name stringclasses 429
values | text stringlengths 0 767k ⌀ |
|---|---|
Bakari Kiango na Juma Issihaka, Mwananchi
mwananchipapers@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Uamuzi wa | Bakari Kiango na Juma Issihaka, Mwananchi
mwananchipapers@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Uamuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kumuondoa Alphayo Kidata kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), umetajwa na wadau kuwa, unalenga kumweka karibu zaidi na Rais kwa ajili ya kumshauri namna ya kuyaenenda masuala ya kikodi.
Ingawa wengine wanayatazama mabadiliko hayo kwa sura hiyo, baadhi ya wadau wameona kilichofanywa na Rais ni kupunguza vita aliyokuwa akipigwa, licha ya kazi nzuri aliyokuwa akiifanya.
Msingi wa hoja hizo ni kauli ya Rais Samia wakati akiwaapisha wateule wake Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar alipomsifu Kidata akisema alifanya vizuri TRA.
Kidata aliyekuwa kamishna wa TRA, juzi Rais Samia amemteuwa kuwa Mshauri wake, huku nafasi yake ikirithiwa na Yusuph Mwenda aliyekuwa bosi wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRA).
“TRA chini ya Kidata imefanya vizuri sana, mapato yameongezeka, sitegemee kama utashuka. Nilimuondoa Kidata niliona mwisho atadata.
“Kazi amefanya vizuri sana niliona mwisho atadata, sasa nakupeleka kijana mtoto wa mjini uhuni wote wa TRA umefanywa na wewe humo humo,” alisema Rais Samia jana alipowaapisha wateule hao.
Kutokana na kauli hiyo ya Rais Samia, Mwananchi jana limezungumza na Mhadhiri wa Biashara wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Omar Mbura aliyetaja sura mbili zinazobeba uamuzi wa Rais kumuondoa Kidata TRA.
Pamoja na ufanisi ulioonyeshwa na Kidata katika utendaji wake, alieleza kuondolewa kwake kumelenga kuwekwa karibu zaidi na mkuu wa nchi ili amshauri kuhusu masuala ya kikodi.
“Kama tunavyoona wakati huu kuna changamoto nyingi za wafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi, Rais alihitaji mtu wa kuwa naye karibu kwa ajili ya kumshauri namna ya kuyaenenda mambo hayo,” alisema.
Kwa mtazamo wa Profesa Mbura, Kidata hakuondolewa isipokuwa amewekwa karibu na Rais ashauri na asimamie utekelezaji, hivyo bado yupo lakini kwa nafasi ya ushauri.
Kwa upande wa Mwenda, alisema kuteuliwa kwake ni baada ya kujaribiwa visiwani Zanzibar na kuonyesha umahiri kiasi cha kuongeza mapato.
“Kwa taarifa zilizopo Zanzibar imeongeza mapato yake maradufu, hiyo ni kazi ya Mwenda, kama alikwenda kule kupimwa basi amepimika na amethibitisha uwezo wake, kwa hiyo anakwenda kusimamia eneo kubwa zaidi huku Kidata akisimama kumshauri,” alisema.
Mtazamo wa Profesa Mbura unashabihiana na kilichoelezwa na Mhadhiri wa Fedha, Uhasibu na Kodi wa Chuo cha Serikali za Mitaa Dodoma, Charles Matekele aliyesema anadhani uamuzi huo umelenga kumweka Kidata karibu zaidi na Rais.
Ukaribu huo kwa mujibu wa Matekele, utarahisisha ushauri kuhusu masuala ya kikodi ambayo kimsingi hayatoki TRA pekee, hata katika halmashauri.
“Katika kuboresha utendaji wa TRA atakuwa anapata ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa mtu aliyewahi kuwepo katika mamlaka hiyo,” alisema.
Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Bara, Issihaka Mchinjita alisema kauli hiyo ya Rais inaashiria changamoto ya kuwajibishana ndani ya Serikali.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, haiwezekani anayedaiwa kufanya vizuri umuondoe, akidai kuho ni kuoneana haya.
Kwa mujibu wa Mchinjita, katika mazingira ya kawaida anayefanya vizuri, mara nyingi huachwa kwenye nafasi yake ili aboreshe zaidi.
Rais wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Vincent Minja alisema Rais ana sababu nyingi za kumuondoa mtu kwenye wadhifa wake.
Lakini, alisema kinachoangaliwa na chemba hiyo ni iwapo Mwenda atakuwa na manufaa kwa wafanyabiashara.
“Tunachoangalia uteuzi huu uliokuja una manufaa kwetu wafanyabiashara au hauna manufaa, kama anavyosema sisi tunaona amemuondoa….
“Unajua unaweza ukawa mzuri lakini ukawa unapigwa vita yule aliyekuteuwa anaamua akuondoe ili msiendelee kupigana vita,” alisema.
Alichokisema Rais
Rais Samia alisema kwa kiasi fulani bosi huyo wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRA) alijitahidi kunyanyua mapato ya Zanzibar na kwamba hivi sasa anapelekwa TRA.
Alimtaka Mwenda kuziba mianya yote ya ukwepaji wa kodi akisema bosi huyo wa TRA anaijua vema kwa sababu alikuwa huko awali.
“Tunakopa tunanyanyasika, twende tukanyanyua za kwetu, Serikali imefanya yote imeweka mazingira mazuri wawekezaji wanakuja, biashara zinafanyika lakini kodi hazilipwi.
“Kariakoo pale tatizo ni kulipa kodi, pale kuna mapato yakikusanywa vizuri kwa mwaka yanaweza kuendesha hata wizara tatu.Lakini mapato hayakusanywi kuingia Serikali, inawezekana yanakusanywa yanaingia mfukoni, nenda kazibe huo mwaya.
Kwa mujibu wa Rais Samia, hivi sasa TRA wanacheza ngoma na kula pilau baada ya Kidata kuondoka na watafurahi endapo Mwenda akifika katika ofisi hizo kwa sababu wanamfahamu.
“Kama unataka kudumu kwa muda Mrefu TRA kageuze uso. Jingine Kidata huyu hakuwa mpenzi hata kwa sisi huku, kwa sababu mzigo wangu unakuja Kidata pitisha mzigo, hapitishi hadi ulipiwe kodi.
“Hawezi kuwa mpenzi wa watu, hata sisi huku tulikuwa hatumpendi kabisa,”
Alimtaka Mwenda kujiandaa na hilo, sio kujifanya mwema kwa kumridhisha kila mtu, “yaani kuwa mzuri kwa sisi, kuwa mzuri kwangu niliyekuteua. Nenda kanikusanyie fedha, ukitaka kumridhisha kila mtu hutafanya kazi.
“Nimemuondosha Kidata anakuja ofisini kwangu kazi yake kubwa kukufuata mgongoni, kwa sababu vichochoro vya TRA anavijua.Sasa hivi msaidizi na mshauri wangu katika ukusanyaji wa mapato.
Alimwambia Mwenda asitake kupendwa bali ahakikishe watu wanalipa kodi, hata ikitokea mtu anaitwa Suluhu anataka kupitisha mzigo au chochote alipe kodi, hakuna kukwepa kodi.
Kuhusu Jafo
Rais Samia alimtaka Dk Jafo kwenda kusikiliza na kutatua kero za za wafanyabiashara na kuhakikisha Kariakoo inafanya kazi saa 24 kwa ushirikiano na taasisi mbalimbali.
Alimtaka Dk Jafo kuhakikisha wafanyabiashara wanakuwa marafiki zake,akisema hataki kusikia wadau hao wanamtafuta waziri hapatikani hasa kama mbunge huyo wa Kisarawe mwenye uwezo wa kuongea na kutembea.
“Ulikuwa ofisi ya Makamu wa Rais, umefanya kazi nzuri, lakini nimeona nikutoe nikupeke biashara maana pilikapilika ni nyingi mno.
“Pale ofisini ulipokuwa ukikaa sitaki ukae, lakini naelewa kwa nini waziri (Dk Kijaji) alikuwa hatoki kwa kazi ninayotaka kukupa ni kushinda Kariakoo panda shuka panda shuka, si rahisi kwa mtoto wa kike na sio kazi rahisi,”alisema.
Rais Samia alimtaka Dk Jafo katika majukumu yake, arejee katika Ilani ya uchaguzi ya CCM inayozungumzia sekta ya biashara na kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binfasi ili kutoa mchango kwa Serikali.
“Lakini ukarejee kauli yangu kuhusu Serikali kuendelea kufanya kila linalowezekana kusikiliza na kutatua changamoto za wafanyabiashara, ndiyo maana nakwambia uwe karibu nao,”alisema.
Rais Samia alisema Kariakoo ndilo eneo zuri la biashara na muhimu kwa biashara, ndilo linalofanya Dar es Salaam, iitwe kitovu cha biashara, mataifa yote yanakwenda Kariakoo.
“Tumewekeza fedha nyingine kujenga masoko yakikamilika huduma zitakuwa saa 24 Kariakoo, nataka ukaifanye Kariakoo itoe huduma saa 24 yenye usalama wa biashara,
“Utakaa vipi na jeshi la polisi au kujipanga hiyo ndio kazi yako, lakini nataka Karikoo liwe soko la Kimataifa, changamoto zilizopo,”alisema.
Mbali na hilo, Rais Samia alifichua kuwa Kariakoo kuna siasa akisema wakati mgomo alituma timu yake kimya kimya kwenda kwa lengo la kuzungumza na wafanyabiashara waliosema hawajui kwa nini wagoma bali wameambiwa kufanya hivyo.
“Tumeambiwa tufunge maduka, tumefunga, tumeambiwa tusiuze hatuuzi, lakini kuna nini ndani hawajui, ukiangalia kwa undani kuna siasa.
“Sasa ili kuondoa siasa, nenda ukakae nao uwasikilize, shida zao na uwasaidie kuzitatua ili Kariakoo kuwa eneo salama la biashara.
Biashara ni ‘field’ viatu unavalia njiani sio kazi ya ofisini,”alisema.
Kuhusu Dk Kijaji Rais Samia alisema anaelewa kulikuwa na uzito fulani ndiyo maana ameamua kumpeleka Ofis ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.
Katika utekelezaji wa jukumu hilo, alimtaka Dk Jafo ahakikishe anakuwa karibu na TRA pamoja na ofisi ya mipango na uwekezaji.
Alimtaka pia Dk Jafo kukaa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila kuangalia na kujipanga kuhusu ujio wa Kariakoo utakuaje ikiwemo masuala ya usalama.
“Lakini pia kuna suala la machinga wanaoleta kero wakati mwingine wanapanga bidhaa zao mbele ya maduka ya watu wengine.
“Kaeni na mkuu wa mkoa (Chalamila) na polisi kujua mnajipangaje kama mtafunga baadhi ya barabara ili usiku wafanyaje biashara, lazima wawapishe wenye maduka wanaolipa kodi,” alisema.
Alimueleza Dk Jafo kuwa kila miezi mitatu anatakiwa ampelekee ripoti kuhusu mwenendo wa biashara Kariakoo na maeneo mengine.
“Dk (Kijaji) nimekupa ahueni na mzigo huu wa biashara najua kwa haya usingeyaweza, nimekupeleka kwenye muungano na mazingira, kama ulisema hazikuhusu sasa yanakuhusu tena utazifanya kazi kweli kweli,”
Rais Samia alimtaka Dk Kijaji kulivalia njuga ajenda za nishati safi ya kupikia. |
Uamuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kumuondoa Alphayo Kidata kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), | Uamuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kumuondoa Alphayo Kidata kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), umetajwa na wadau kuwa, unalenga kumweka karibu zaidi na Rais kwa ajili ya kumshauri namna ya kuyaenenda masuala ya kikodi.
Ingawa wengine wanayatazama mabadiliko hayo kwa sura hiyo, baadhi ya wadau wameona kilichofanywa na Rais ni kupunguza vita aliyokuwa akipigwa, licha ya kazi nzuri aliyokuwa akiifanya.
Msingi wa hoja hizo ni kauli ya Rais Samia wakati akiwaapisha wateule wake Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar alipomsifu Kidata akisema alifanya vizuri TRA.
Kidata aliyekuwa kamishna wa TRA, juzi Rais Samia amemteuwa kuwa Mshauri wake, huku nafasi yake ikirithiwa na Yusuph Mwenda aliyekuwa bosi wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRA).
“TRA chini ya Kidata imefanya vizuri sana, mapato yameongezeka, sitegemee kama utashuka. Nilimuondoa Kidata niliona mwisho atadata.
“Kazi amefanya vizuri sana niliona mwisho atadata, sasa nakupeleka kijana mtoto wa mjini uhuni wote wa TRA umefanywa na wewe humo humo,” alisema Rais Samia jana alipowaapisha wateule hao.
Kutokana na kauli hiyo ya Rais Samia, Mwananchi jana limezungumza na Mhadhiri wa Biashara wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Omar Mbura aliyetaja sura mbili zinazobeba uamuzi wa Rais kumuondoa Kidata TRA.
Pamoja na ufanisi ulioonyeshwa na Kidata katika utendaji wake, alieleza kuondolewa kwake kumelenga kuwekwa karibu zaidi na mkuu wa nchi ili amshauri kuhusu masuala ya kikodi.
“Kama tunavyoona wakati huu kuna changamoto nyingi za wafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi, Rais alihitaji mtu wa kuwa naye karibu kwa ajili ya kumshauri namna ya kuyaenenda mambo hayo,” alisema.
Kwa mtazamo wa Profesa Mbura, Kidata hakuondolewa isipokuwa amewekwa karibu na Rais ashauri na asimamie utekelezaji, hivyo bado yupo lakini kwa nafasi ya ushauri.
Kwa upande wa Mwenda, alisema kuteuliwa kwake ni baada ya kujaribiwa visiwani Zanzibar na kuonyesha umahiri kiasi cha kuongeza mapato.
“Kwa taarifa zilizopo Zanzibar imeongeza mapato yake maradufu, hiyo ni kazi ya Mwenda, kama alikwenda kule kupimwa basi amepimika na amethibitisha uwezo wake, kwa hiyo anakwenda kusimamia eneo kubwa zaidi huku Kidata akisimama kumshauri,” alisema.
Mtazamo wa Profesa Mbura unashabihiana na kilichoelezwa na Mhadhiri wa Fedha, Uhasibu na Kodi wa Chuo cha Serikali za Mitaa Dodoma, Charles Matekele aliyesema anadhani uamuzi huo umelenga kumweka Kidata karibu zaidi na Rais.
Ukaribu huo kwa mujibu wa Matekele, utarahisisha ushauri kuhusu masuala ya kikodi ambayo kimsingi hayatoki TRA pekee, hata katika halmashauri.
“Katika kuboresha utendaji wa TRA atakuwa anapata ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa mtu aliyewahi kuwepo katika mamlaka hiyo,” alisema.
Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Bara, Issihaka Mchinjita alisema kauli hiyo ya Rais inaashiria changamoto ya kuwajibishana ndani ya Serikali.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, haiwezekani anayedaiwa kufanya vizuri umuondoe, akidai kuho ni kuoneana haya.
Kwa mujibu wa Mchinjita, katika mazingira ya kawaida anayefanya vizuri, mara nyingi huachwa kwenye nafasi yake ili aboreshe zaidi.
Rais wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Vincent Minja alisema Rais ana sababu nyingi za kumuondoa mtu kwenye wadhifa wake.
Lakini, alisema kinachoangaliwa na chemba hiyo ni iwapo Mwenda atakuwa na manufaa kwa wafanyabiashara.
“Tunachoangalia uteuzi huu uliokuja una manufaa kwetu wafanyabiashara au hauna manufaa, kama anavyosema sisi tunaona amemuondoa….
“Unajua unaweza ukawa mzuri lakini ukawa unapigwa vita yule aliyekuteuwa anaamua akuondoe ili msiendelee kupigana vita,” alisema.
Alichokisema Rais
Rais Samia alisema kwa kiasi fulani bosi huyo wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRA) alijitahidi kunyanyua mapato ya Zanzibar na kwamba hivi sasa anapelekwa TRA.
Alimtaka Mwenda kuziba mianya yote ya ukwepaji wa kodi akisema bosi huyo wa TRA anaijua vema kwa sababu alikuwa huko awali.
“Tunakopa tunanyanyasika, twende tukanyanyua za kwetu, Serikali imefanya yote imeweka mazingira mazuri wawekezaji wanakuja, biashara zinafanyika lakini kodi hazilipwi.
“Kariakoo pale tatizo ni kulipa kodi, pale kuna mapato yakikusanywa vizuri kwa mwaka yanaweza kuendesha hata wizara tatu.Lakini mapato hayakusanywi kuingia Serikali, inawezekana yanakusanywa yanaingia mfukoni, nenda kazibe huo mwaya.
Kwa mujibu wa Rais Samia, hivi sasa TRA wanacheza ngoma na kula pilau baada ya Kidata kuondoka na watafurahi endapo Mwenda akifika katika ofisi hizo kwa sababu wanamfahamu.
“Kama unataka kudumu kwa muda Mrefu TRA kageuze uso. Jingine Kidata huyu hakuwa mpenzi hata kwa sisi huku, kwa sababu mzigo wangu unakuja Kidata pitisha mzigo, hapitishi hadi ulipiwe kodi.
“Hawezi kuwa mpenzi wa watu, hata sisi huku tulikuwa hatumpendi kabisa,”
Alimtaka Mwenda kujiandaa na hilo, sio kujifanya mwema kwa kumridhisha kila mtu, “yaani kuwa mzuri kwa sisi, kuwa mzuri kwangu niliyekuteua. Nenda kanikusanyie fedha, ukitaka kumridhisha kila mtu hutafanya kazi.
“Nimemuondosha Kidata anakuja ofisini kwangu kazi yake kubwa kukufuata mgongoni, kwa sababu vichochoro vya TRA anavijua.Sasa hivi msaidizi na mshauri wangu katika ukusanyaji wa mapato.
Alimwambia Mwenda asitake kupendwa bali ahakikishe watu wanalipa kodi, hata ikitokea mtu anaitwa Suluhu anataka kupitisha mzigo au chochote alipe kodi, hakuna kukwepa kodi.
Kuhusu Jafo
Rais Samia alimtaka Dk Jafo kwenda kusikiliza na kutatua kero za za wafanyabiashara na kuhakikisha Kariakoo inafanya kazi saa 24 kwa ushirikiano na taasisi mbalimbali.
Alimtaka Dk Jafo kuhakikisha wafanyabiashara wanakuwa marafiki zake,akisema hataki kusikia wadau hao wanamtafuta waziri hapatikani hasa kama mbunge huyo wa Kisarawe mwenye uwezo wa kuongea na kutembea.
“Ulikuwa ofisi ya Makamu wa Rais, umefanya kazi nzuri, lakini nimeona nikutoe nikupeke biashara maana pilikapilika ni nyingi mno.
“Pale ofisini ulipokuwa ukikaa sitaki ukae, lakini naelewa kwa nini waziri (Dk Kijaji) alikuwa hatoki kwa kazi ninayotaka kukupa ni kushinda Kariakoo panda shuka panda shuka, si rahisi kwa mtoto wa kike na sio kazi rahisi,”alisema.
Rais Samia alimtaka Dk Jafo katika majukumu yake, arejee katika Ilani ya uchaguzi ya CCM inayozungumzia sekta ya biashara na kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binfasi ili kutoa mchango kwa Serikali.
“Lakini ukarejee kauli yangu kuhusu Serikali kuendelea kufanya kila linalowezekana kusikiliza na kutatua changamoto za wafanyabiashara, ndiyo maana nakwambia uwe karibu nao,”alisema.
Rais Samia alisema Kariakoo ndilo eneo zuri la biashara na muhimu kwa biashara, ndilo linalofanya Dar es Salaam, iitwe kitovu cha biashara, mataifa yote yanakwenda Kariakoo.
“Tumewekeza fedha nyingine kujenga masoko yakikamilika huduma zitakuwa saa 24 Kariakoo, nataka ukaifanye Kariakoo itoe huduma saa 24 yenye usalama wa biashara,
“Utakaa vipi na jeshi la polisi au kujipanga hiyo ndio kazi yako, lakini nataka Karikoo liwe soko la Kimataifa, changamoto zilizopo,”alisema.
Mbali na hilo, Rais Samia alifichua kuwa Kariakoo kuna siasa akisema wakati mgomo alituma timu yake kimya kimya kwenda kwa lengo la kuzungumza na wafanyabiashara waliosema hawajui kwa nini wagoma bali wameambiwa kufanya hivyo.
“Tumeambiwa tufunge maduka, tumefunga, tumeambiwa tusiuze hatuuzi, lakini kuna nini ndani hawajui, ukiangalia kwa undani kuna siasa.
“Sasa ili kuondoa siasa, nenda ukakae nao uwasikilize, shida zao na uwasaidie kuzitatua ili Kariakoo kuwa eneo salama la biashara.
Biashara ni ‘field’ viatu unavalia njiani sio kazi ya ofisini,”alisema.
Kuhusu Dk Kijaji Rais Samia alisema anaelewa kulikuwa na uzito fulani ndiyo maana ameamua kumpeleka Ofis ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.
Katika utekelezaji wa jukumu hilo, alimtaka Dk Jafo ahakikishe anakuwa karibu na TRA pamoja na ofisi ya mipango na uwekezaji.
Alimtaka pia Dk Jafo kukaa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila kuangalia na kujipanga kuhusu ujio wa Kariakoo utakuaje ikiwemo masuala ya usalama.
“Lakini pia kuna suala la machinga wanaoleta kero wakati mwingine wanapanga bidhaa zao mbele ya maduka ya watu wengine.
“Kaeni na mkuu wa mkoa (Chalamila) na polisi kujua mnajipangaje kama mtafunga baadhi ya barabara ili usiku wafanyaje biashara, lazima wawapishe wenye maduka wanaolipa kodi,” alisema.
Alimueleza Dk Jafo kuwa kila miezi mitatu anatakiwa ampelekee ripoti kuhusu mwenendo wa biashara Kariakoo na maeneo mengine.
“Dk (Kijaji) nimekupa ahueni na mzigo huu wa biashara najua kwa haya usingeyaweza, nimekupeleka kwenye muungano na mazingira, kama ulisema hazikuhusu sasa yanakuhusu tena utazifanya kazi kweli kweli,”
Rais Samia alimtaka Dk Kijaji kulivalia njuga ajenda za nishati safi ya kupikia. |
Muda wa zabuni iliyotangazwa ya kumsaka mkandarasi atakayekifanyia matengenezo makubwa kivuko cha MV | Muda wa zabuni iliyotangazwa ya kumsaka mkandarasi atakayekifanyia matengenezo makubwa kivuko cha MV Kigamboni umefika mwisho, huku kampuni mbili za Tanzania zikiomba kazi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya zabuni hiyo yenye namba X8/2023/2024/W/53 mkandarasi aliyehitajika ni yule atakayekuwa na uwezo wa kufanya ukarabati mkubwa wa kivuko hicho, kwa maana kubadilisha zaidi ya asilimia 90 ya vifaa vilivyomo, zikiwemo injini nne.
Hatua ya kutangazwa kwa zabuni hiyo, ilitokana na kivuko hicho kusimamishwa kutoa huduma na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), baada ya kupitiliza muda wa kufanyiwa matengenezo makubwa.
Mzizi wa yote hayo ni ripoti maalumu iliyoandikwa na Gazeti la Mwananchi kuanzia Mei 25, mwaka huu ikibainisha kivuko hicho na vingine, vilipitiliza muda wa matengenezo makubwa na hivyo kuhatarisha usalama wa watumiaji.
Juni 7, mwaka huu, Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (Temesa), ilitangaza kusitisha huduma za kivuko hicho, kwa kile ilichofafanua kuwa, kinakwenda kufanyiwa matengenezo makubwa.
Katika taarifa hiyo, Temesa ilisema huduma za uvushaji Kigamboni-Magogoni zitaendelea kutolewa na kivuko cha MV Kazi na Sea Tax za kampuni ya Azam Marine Ltd.
Baada ya hatua hiyo Mwananchi jana ilimtafuta Meneja wa Vivuko Kanda ya Mashariki wa Temesa, Abdulrahman Ameir aliyesema zabuni ya kumpata mkandarasi wa kufanya matengenezo makubwa ya kivuko hicho ilishatangazwa.
Kwa mujibu wa Ameir, tayari kampuni mbili kutoka Tanzania zimeomba zabuni hiyo na hana uhakika iwapo tayari mchakato wa kukabidhiwa kazi hiyo umekamilika au laa.
"Waliomba wazabuni wawili kampuni za Tanzania na nafikiri hivi karibuni mmoja atakabidhiwa kazi kwa ajili ya kwenda kwenye matengenezo hayo," alisema.
Hata hivyo, Mwananchi linazo taarifa za uhakika kuwa, bado mzabuni wa kufanya matengenezo ya kivuko hicho hajatangazwa ingawa kampuni mbili zimeshaomba kazi hiyo.
Kadhalika, gazeti hili linazo taarifa za uhakika kuwa, kampuni ya Songoro Marine Ltd ni miongoni mwa hizo mbili zilizoomba kazi hiyo ya kuifanyia matengenezo makubwa MV Kigamboni.
Katika zabuni ya matengenezo makubwa ya kivuko hicho yenye namba X8/2023/2024/W/53, mwisho wa kutuma maombi ilikuwa Julai 1, mwaka huu.
Chanzo cha ndani ya Temesa kimeieleza Mwananchi kuwa, wiki ijayo mzabuni atatangazwa na anatarajiwa akafanye kazi kwa miezi isiyozidi 10, hivyo mapema mwakani kivuko kitarejea.
Sekta binafsi hiyooo…
Wakati abiria wakitaabika na uhaba wa vivuko, baada ya MV Kigamboni na Magogoni kutokuwepo kwa sababu ya matengenezo hayo, kampuni ya Azam Marine Ltd ipo mbioni kutoa huduma za uvushaji.
Taarifa kutoka katika chanzo kinachoaminika, zinaeleza kampuni hiyo imekubali kutoa huduma baada ya Serikali kulegeza masharti na kuiruhusu itoze Sh500 kama nauli kwa abiria watakaovushwa na vivuko vyake.
Awali, kikwazo cha uwekezaji huo kilitokana na Serikali kuitaka kampuni hiyo itoze nauli isiyozidi Sh300 na hivyo Azam Marine Ltd kuona haina maslahi kibiashara.
Katika mazungumzo kati ya kampuni hiyo, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na Temesa, Azam Marine iliahidi kuwasilisha pendekezo lake la kufanya uwekezaji katika eneo hilo.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kampuni hiyo, kinaeleza wapo katika hatua za mwisho za makubaliano na kwamba kabla ya Julai kuisha pengine mikataba ukasainiwa.
Baada ya kusainiwa kwa mikataba huo, Azam Marine Ltd itafanya ujenzi wa pande zote mbili kwa ajili ya maegesho ya boti zitakazotoa huduma na maeneo ya abiria kukaa na kupanda.
“Pia zitachongwa boti mbili au tatu ambazo ndizo zitakazotoa huduma ya uvushaji katika eneo la Magogoni-Kivukoni,” kilieleza chanzo hicho.
Kilipoulizwa ni muda gani unahitajika kukamilisha uchongaji wa boti hizo, chanzo hicho kilisema baada ya siku ya kupewa mkataba miezi minne hadi mitano itatosha kulikamilisha hilo. |
Lilikuwa suala la muda tu, kwa Mchungaji Peter Msigwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndivyo | Lilikuwa suala la muda tu, kwa Mchungaji Peter Msigwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndivyo unavyoweza kueleza baada ya kada huyo wa zamani wa Chadema kutimkia katika chama hicho tawala.
Kwa mujibu wa wanazuoni na wanasiasa, uamuzi wa Msigwa kuihama Chadema na kujiunga na CCM ulitarajiwa, kutokana na mienendo yake ndani ya chama hicho cha upinzani.
Msigwa ametambulishwa kuwa mwanachama mpya wa CCM jana, mbele ya wajumbe wa halmashauri kuu ya chama hicho (NEC), katika kikao kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Uamuzi wa mwanasiasa huyo umethibitisha tetesi zilizokuwa zikiibuliwa mara kwa mara na wadau zikimnasibisha Mchungaji Msigwa na CCM tangu enzi za utawala wa Hayati John Magufuli.
Mei mwaka huu, wakati anatangaza kukata rufaa baada ya matokeo ya uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa, Msigwa alisema mifumo ya chama imetumika kumhujumu asishinde, kitendo kinaifanya Chadema kukosa uhalali wa kuikosoa CCM.
“Kama Chadema tunalalamikia Serikali ya CCM haitendi haki katika kusimamia uchaguzi, tulitakiwa tuwe mfano wa kuigwa lakini kati8ka chaguzi zetu haki haitendeki.
“Hali hii inaleta mashaka na harufu ya uvundo wa ukiukwaji mkubwa wa haki ndani ya Chadema ambacho kinatakiwa kiwe mstari wa mbele katika demokrasia,” aliwahi kusema Msigwa.
Hata Machi mwaka 2020, alipohukumiwa kwenda jela au kulipa faini katika kesi iliyokuwa ikimkabili yeye na viongozi wengine saba wa Chadema, Sh38 milioni alilipiwa na Hayati Magufuli, kati ya Sh40 milioni zilizohitajika.
Sambamba hilo, Msigwa alifuatwa na gari za Serikali na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM wa wakati huo, Humphrey Polepole, jambo ambalo liliongeza dhana za nasaba yake na chama tawala. Hata hivyo, Msigwa aligoma kupanda gari hilo, badala yake aliondoka kwa gari la wakili wa Chadema.
Chadema: Intelejensia zilijua
Uamuzi wa Msigwa kujiunga na CCM lilikuwa suala linalosubiri muda tu, kama inavyoelezwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itifaki, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema.
Katika hoja yake hiyo, Mrema alisema intelejensia ya Chadema ilishatoa taarifa mwenendo wake na kulikuwa na dalili zote za Msigwa kujiunga na chama tawala.
“Tulikuwa tunasubiri muda ufike na muda umefika leo, kwa sababu ameamua kwenda CCM, tunaendelea kukijenga chama chetu,” alisema.
Mrema alizihusisha harakati za Msigwa katika siku za mwisho mwisho ndani ya Chadema na vurugu za maandalizi ya kupandisha thamani yake ili aondokea.
Katika msisitizo wa kauli yake hiyo, alisema: “Hata uko CCM Mchungaji Msigwa akikosa cheo ataondoka.”
Kuhusu rufaa yake ya kupinga ushindi dhidi ya Sugu, Mrema alisema ilikuwa isikilizwe katika kikao cha Baraza Kuu, kwa sababu mwanasiasa huyo alikuwa mjumbe wa kamati kuu.
“Tulikuwa tunasubiri chaguzi zote zimalizike ndipo tuitishe baraza kuu kujadili rufaa ya Msigwa, tusingeweza kujadili rufaa yake pekee maana huenda zingine zingejitokeza na kufanya vikao mara kwa mara vya baraza kuu ni gharama,” alisema Mrema.
Kwa uamuzi huo wa Msigwa, alisema mchakato wa kusikiliza rufaa yake utakuwa umejifia hapo.
Uamuzi wa Msigwa, umemuumiza Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema aliyesema angetamani kubaki kuwa naye ndani ya chama hicho.
“Nilitamani tuendelee naye kufanya kazi, lakini ni uamuzi wa mtu huwezi kuuzuia, Msigwa alikuwa ni kama kaka yangu, nilitamani tuendelea kuwa timu moja (Chadema),” alisema Lema ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema kama alivyokuwa Msigwa zamani.
Haikushtua
Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Conrad Masabo alisema si jambo linaloshtua kwa Msigwa kufanya uamuzi huo.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, tayari kulikuwa na tetesi na hisia juu ya alichokiamua na matukio kadhaa yaliakisi matarajio hayo.
Matukio hayo kwa mujibu wa Dk Masabo, ni tuhuma za rushwa zilizoibuliwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu, ambazo ingawa Msigwa hakutajwa moja kwa moja, lakini ujumbe ulionekana kumhusu.
“Lissu alianza kutoa malalamiko ya fedha za CCM kuivuruga Chadema akiwa Iringa, hii maana yake watu wa Iringa walipata mgawo wa fedha hizo na haiwezi kugawiwa fedha kwenye Mkoa Mwenyekiti asihusike,” alisema.
Tuhuma hizo sio za kwanza, alisema Msigwa aliwahi kukumbwa na tuhuma za unasibu na CCM tangu enzi za utawala wa Hayati John Magufuli.
Si pigo kwa Chadema wala turufu kwa CCM
Hata hivyo, mwanazuoni huyo alieleza uamuzi huo wa Msigwa si pigo kwa Chadema wala turufu kwa CCM.
Hilo linatokana na kile alichoeleza, Msigwa hakuwa tishio kwa CCM kabla ya kujiunga nacho, lakini hakuwa mwanachama anayetegemewa zaidi ndani ya Chadema.
Kwa mtazamo wa Dk Masabo, uamuzi wa mwanasiasa huyo pengine umechagizwa ama na ahadi ya nafasi ya uongozi serikalini au ameshindwa kuvumilia tuhuma dhidi yake.
Sambamba na hilo, alisema kingine kinachoweza kuwa sababu ya kuondoka kwake ni hatua yake ya kukosa uenyekiti wa kanda ya Nyasa, ambao ungemuondolea sifa ya kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu.
“Angekuwa katika hali ngumu katika chama (Chadema) na hata uwezekano wa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama usingekuwepo, angebaki kuwa mwanachama wa kawaida.
“Ulikuwa mjumbe wa kamati kuu na sasa unaenda kuwa mwanachama wa kawaida inahitaji uwe umeiva sana kisiasa ili kuimudu hali hiyo,” alisisitiza.
Kwa uamuzi wake huo, Dk Masabo alisema amezidi kujiweka kwenye nyakati ngumu kwa sababu haionekani nafasi ambayo Msigwa atapewa kuwaondoa waliopo sasa.
“Kwa ubunge itamuiya vigumu kwa sababu kwanza ndani ya CCM yenyewe nani utamtoa umuweke Msigwa, pia hakuwa tishio kwa CCM, labda nafasi nyingine,” alisema.
Hatua ya kuondoka kwake Chadema, alieleza kunampa nguvu Lissu ya kumsema vizuri kuhusu tuhuma za rushwa na pengine, uamuzi huo unalithibitisha hilo.
Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Richard Mbunda aliungana na wadau wengine akisema lilikuwa ni suala muda kwa mwanasiasa huyo kuhamisa CCM hasa baada ya kushindwa uchaguzi wa Kanda ya Nyasa dhidi ya Sugu.
“Lilikuwa ni suala la muda tu, ni sawa kama vile unavyomzungumzia Mpina (Luhaga) halafu ukasikia amehamia Chadema au vyama vingine vya upinzani,” alisema.
Dalili za kuondoka kwake kwa mujibu wa Dk Mbunda, zilianza kujitokeza pale alipokuwa akilalamika kuhusu mwenendo wa uchaguzi wa kanda ya Nyasa akidai kuhujumiwa.
“Ni wazi kwamba alikuwa na kinyongo kwamba hakushindwa kihalali, Msigwa ni mwanasiasa machachali anayetaka kuendelea kubaki katika mstari wa siasa, sasa ukianguka katika chama unachotakiwa kufanya siasa itakula kwako.
“Nadhani Msigwa atakuwa ameshafuatwa mara nyingi sana na CCM, sasa alivyoona nafasi hii ameitumia. Ni kitu kilichotarajiwa hasa baada ya kushindwa uenyekiti wa Nyasa,” alisema Dk Mbunda.
Wananchi Iringa
Uamuzi wa Msigwa kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chadema Manispaa ya Iringa Frank Nyalusi, umeacha pengo ndani ya chama hicho, lakini alichokifanya ametimiza haki yake ya msingi kikatiba.
“Nikisema kuondoka kwa Msigwa hakujaacha pengo lolote nitakuwa muongo, amekuwa mbunge vipindi viwili, mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na kiongozi wa Kanda ya Nyasa, ameacha pengo lakini ametimiza haki ya msingi ya kikatiba ,” alisema.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Joseph Lyata ambaye awali alikuwa Diwani wa Kata ya Kwakilosa na Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa kupitia Chadema alisema mwanasiasa huyo amefanya maamuzi ya msingi.
“Ni haki ya kila Mtanzania kuchagua chama anachopenda, hiyo ni haki yake ya msingi kabisa. Hakuna anayemzuia mtu kuchagua chama anachopenda,” alisema.
Lakini, kada wa Chadema anayeishi Frelimo mkoani Iringa anaona Msigwa alipaswa kuvumilia, badala ya kufanya maamuzi hayo.
“Nimepata mshtuko kusikia amehamia CCM, angevumilia tu kwa sababu kwenye siasa kuna mambo mengi ambayo ni ya kawaida, hata huko CCM atakutana na pilika pilika kama alizokutana nazo Chadema,” alisema Ndonde. |
Ukimya katika taarifa za mwenendo wa tuhuma za aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk Yahaya Nawanda u | Ukimya katika taarifa za mwenendo wa tuhuma za aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk Yahaya Nawanda umewashtua wadau wa sheria, wakitaka upelelezi uharakishwe ili mtuhumiwa afikishwe mahakamani.
Msisitizo wa wataalamu hao wa taaluma ya sheria, unatokana na kile walichofafanua, ni mahakama pekee ndiyo yenye mamlaka ya kuamua ama mtuhumiwa ana hatia au vinginevyo.
Mzizi wa hoja za wadau hao ni ukimya uliotawala katika mwenendo wa ushughulikiwaji wa tuhuma za Dk Nawanda tangu Jeshi la Polisi lilipotangaza kumkamata Juni 13, mwaka huu.
Dk Nawanda anatuhumiwa kumlawiti mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT) mkoani Mwanza na baadaye Juni 11, Rais Samia Suluhu Hassan alitengua uteuzi wake na kurithiwa na Kenani Kihongosi.
Taarifa ya Juni 13, ndiyo iliyokuwa ya mwisho kwa jeshi hilo kuitoa kwa umma, baada ya hapo hakukuwa na mwendelezo wa taarifa yoyote na hata walipotafutwa ilikuwa vigumu kuzungumzia.
Mara ya mwisho Mwananchi ilizungumza na Msemaji wa jeshi hilo, David Misime kutaka kujua iwapo mtuhumiwa huyo anaendelea kushikiliwa mahabusu au yupo nje kwa dhamana, alijibu kwa ufupi, “Subirini.”
Hata hivyo, gazeti hili linazo taarifa za uhakika kuwa, Dk Nawanda yupo nje muda mrefu kwa dhamana na bado hakupelekwa mahakamani hadi sasa.
Hatua hiyo imewatia wasiwasi wadau hao, wakidhani kunaweza kutokea masuala ya kesi kumalizwa kifamilia.
Msingi wa hofu za wadau hao ni kuwepo kwa tabia za kesi zinazohusisha ulawiti kumalizwa kifamilia kama ilivyowahi kuelezwa katika ripoti ya utafiti wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na watoto (UNICEF) mwaka 2017.
Utafiti huo, unabainisha kesi nyingi za ukatili wa kingono dhidi ya watoto humalizwa katika mazingira ya nyumbani.
Nayo Ripoti ya Haki za Binadamu kwa Mwaka 2022 iliyotolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) mapema mwaka 2023 ilitaja “utamaduni wa kusameheana” na “kuficha aibu ya familia” kama moja ya sababu zinazochochea vitendo vya ukatili dhidi ya watoto Tanzania.
Hata hivyo, tathmini ya LHRC, ilibinisha kati ya kesi 100 za ulawiti na ubakaji zinazoripotiwa polisi, ni 15 tu ndiyo hufikishwa mahakamani.
Wasemavyo wadau
Ingawa hatua ya mtuhumiwa huyo kuwa nje kwa dhamana ni haki yake, kulipaswa kutolewa taarifa kwa umma kuhusu mwenendo wa kesi yake kama inavyoelezwa na Mkurugenzi wa Uchechemuzi na Maboresho wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Fulgence Massawe.
Taarifa hiyo kwa umma, alisema ilipaswa kueleza kila hatua inayofikiwa kuhusu tuhuma zake.
Kwanini ni muhimu taarifa hizo kutolewa, Massawe alisema kwa sababu mtuhumiwa ni mtu maarufu na alikuwa kiongozi mkubwa serikalini, hivyo jamii inastahili kuarifiwa hatua zote.
“Ujue Mkuu wa Mkoa ni mwakilishi wa Rais katika ngazi ya mkoa, ni kiongozi mkubwa na mwenendo wa kesi anayotuhumiwa nayo ulipaswa kutolewa taarifa kila hatua,” alisisitiza.
Pamoja na mtazamo wake huo, Massawe alipendekeza kuharakishwa kwa upelelezi ili kama mtuhumiwa ana hatia afikishwe mahakamani kwa ajili ya hatua nyingine za kisheria.
Mtaalamu wa masuala ya sheria, Frank Chundu alielekeza hoja yake katika changamoto za upelelezi, akisema ni hatua ambayo kwa Tanzania haina kikomo na hivyo kusababisha mamlaka zinazohusika zisione haja ya kuharakisha.
Utaratibu huo, alisema unasababisha kutotendwa haki akifafanua katika baadhi kesi watuhumiwa wanawekwa mahabusu muda mrefu.
“Kwenye hili la jamii inahitaji kujua nini kinaendelea, bado Polisi hawaoni kama wana wajibu wa kufanya uchunguzi na upelelezi haraka,” alisema.
Kwa mujibu wa wakili huyo, kesi hiyo inafuatiliwa na jamii ili kujua iwapo haki inatendeka kwa makundi yote, yaani wananchi na hata viongozi.
“Polisi kama kawaida yao kwenye mambo yanayowahitaji wafanye uchunguzi wamekuwa wazito kuchukua hatua na hiyo sio kesi moja ni nyingi,” alisema.
Kwa kadri upelelezi unavyochelewa, alieleza ndivyo makali ya kesi yanavyopungua.
Hata hivyo, alisema ingawa sheria haijaweka ukomo wa upelelezi, Jeshi la Polisi linawajibika kufanya uchunguzi kwa wakati kama msingi wa utendaji haki.
“Mahakama ndiyo inayopaswa kuamua kwamba ametenda au hajatenda, hakuna sababu ya Polisi kuendelea kukaa na mtuhumiwa au aendelee kuripoti kwao kama kawaida. Watu wameathirika wanataka kuona haki ikitendeka,” alisema.
Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Ole Ngurumwa alisema kwa sababu taarifa ya awali ilihusisha tuhuma zilizokuwa wazi na mahakama ndiyo yenye mamlaka ya kuamua ama za kweli au vinginevyo.
Kwa sababu hiyo, Ole Ngurumwa alitaka kesi ifikishwe mahakamani ili ijulikane kama tuhuma dhidi ya Dk Nawanda ni za kweli au hapana.
“Kitendo cha kutaka kumalizia kesi bila kwenda mahakamani ni kuvunja utaratibu wa utawala wa sheria,” alisema.
Mtaalamu mwingine wa masuala ya sheria, Hekima Mwasipu alisema
Wakili Hekima Mwasipu alisema kukosekana ukomo wa muda wa upelelezi katika makosa ya jinai, kusifanye Polisi washindwe kutimiza wajibu wao wa kukamilisha uchunguzi.
Kwa sababu jeshi hilo kwa sasa lina vifaa vya kisayansi, alitaka upelelezi ufanywe haraka ili kuhitimisha jambo hilo.
Hata hivyo, wakili huyo alionyesha mashaka katika kuchelewa kwa upelelezi huo, kwa kile alichoeleza inawezekanaje uchelewe ilhali aliyefanyiwa yupo.
“Hata Rais Samia Suluhu Hassan wakati anapokea ripoti ya Tume ya Haki Jinai alieleza suala la upelelezi limekuwa changamoto, nafikiri ni wakati wa kufanyia kazi mapendekezo ya ripoti ili kutatua hizi kasoro zilizopo wazi,” alisema.
Kwa mujibu wa Wakili Mwasipu, inashangaza kesi zilizopo wazi zinachukua muda mrefu kama zile ambazo ushahidi wake umejificha.
“Hapa tunakuwa hatutendi haki kwa wale ambao wanakuwa wametendewa hayo makosa,” alisema wakili huyo.
Mwanaharakati wa haki za binadamu, Dk Ananilea Nkya alisema kwa kadri Polisi wanavyochelewa kumpeleka mahakamani wanasababisha umma uamini kuwa sheria zimetungwa kwa ajili ya wananchi mafukara na si viongozi.
“Polisi wanavyoendelea kuchelewesha kumpeleka mahakamani umma unachikilia kwamba Sheria zimetungwa kwa ajili ya wananchi mafukara na siyo viongozi,” alisema.
Alisisitiza sheria inapaswa kuchukua mkondo wake maana kosa lililofanywa ni jinai.
“Kosa la jinai ni kosa dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa hiyo polisi wanatakiwa kumfikisha mahakamani haraka iwezekanavyo,” alisisitiza. |
Utoaji wa miradi mbadala ya kujikimu kiuchumi kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi | Utoaji wa miradi mbadala ya kujikimu kiuchumi kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi ni moja ya hatua iliyopendekezwa kukomesha uharibifu wa hifadhi nchini.
Hatua hiyo pia, imetajwa kusaidia kupunguza au kukomesha kabisa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyofanywa dhidi ya wananchi wanaoishi pembezoni mwa maeneo hayo, yakiwemo mauaji na kuwahamisha kwa mabavu.
Pendekezo hilo ni moja kati ya 10, yaliyotolewa katika Ripoti ya Hali ya Haki za binadamu katika sekta ya uhifadhi Tanzania, ikihusisha mikoa yote nchini mwaka 2024.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, iliyotolewa na Taasisi ya Centre for Strategic Litigation (CSL) kwa kushirikiana na Shirika la Kutetea Utawala wa Sheria na Media Brain, SK Media, ulinzi wa hifadhi unafanywa bila kuzingatia haki za binadamu.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana, kunapaswa kuundwa tume ya kuchunguza ukiukwaji wa haki za binadamu kuhusiana na uhifadhi.
“Lengo la hatua hii ni kutoa mapendekezo juu ya sera na marekebisho ya kisheria pamoja na mabadiliko katika mfumo wa kisheria wa uhifadhi wa nchi,” imeeleza sehemu ya ripoti hiyo.
Pendekezo lingine ni watumishi wanaofanya kazi katika maeneo ya hifadhi kujengewa uwezo juu ya kuzingatia haki za binadamu, ili wajiepushe na vitendo visivyofaa dhidi ya wananchi.
Kama hiyo haitoshi, ripoti hiyo imependekeza kuwajibishwa kwa watumishi hao wanaokiuka haki za binadamu, pale itakapochunguzwa na kubainika wamekiuka.
“Serikali iongeze juhudi za mawasiliano zinazolenga kuongeza imani ya umma, ushiriki na ushirikiano katika uhifadhi wa maliasili,” ilieleza ripoti hiyo.
Ripoti hiyo, imependekeza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ihakikishe inazingatia kanuni na miongozo ya msingi ya Umoja wa Mataifa kuhusu uhamishaji na uhamishaji wa watu kwa maendeleo.
Pendekezo lingine ni kwa Wizara ya Maliasili na Utalii iangalie upya marufuku ya usafirishaji wa mazao ya misitu ili kuimarisha uhifadhi miongoni mwa jamii zinazojihusisha na biashara hiyo.
“Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi (Zanzibar) iimarisha mazungumzo na wadau ili kubaini changamoto katika uhifadhi wa bahari huku ikitoa na kuongeza elimu na uhamasishaji juu ya uhifadhi wa bahari,” ilieleza.
Mashirika ya kiraia nayo, yalitakiwa kuongeza juhudi za kutoa elimu na msaada wa kisheria na kampeni za uhamasishaji wa kisheria kwa jamii kwa kushirikiana na Serikali.
Akizungumza katika uzinduzi wa ripoti hiyo, Mkurugenzi wa Centre for Strategic Litigation (CSL), Deusdedit Rweyemamu alisema pamoja na sekta ya utalii na uhifadhi kuwa na mchango katika maendeleo nchini, ni vema usimamizi wake usihusishe kuvunja haki za binadamu.
Katika maelezo yake, alisema mhifadhi wa asili wa hifadhi zote nchini ni mwananchi kwa kuwa amekuwa akiishi katika eneo hilo kabla ya kuwa hifadhi.
Kinachohitajika, alisema ni mazungumzo mazuri na kuwekewa mazingira bora ili raia waendelee kuzihifadhi hifadhi hizo,. Badala ya kuziharibu.
“Mjadala unaohitajika ni namna gani tunatambua haki za wahifadhi wa asili ambao kwa mujibu wa tafsiri yangu ni binadamu walioanza kuishi kabla ya kutambulika kwa hifadhi husika,” alisema.
Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini, Tom Nyanduga alisema aghalabu utunzaji wa hifadhi Tanzania umekuwa ukimlinda mnyama na kukiuka haki za binadamu.
“Uhifadhi huo umeshindwa kujibu changamoto wanazokumbana nazo jamii za kitanzania zinazoishi pembezoni mwa hifadhi,” alisema.
Alieleza ndani ya ripoti hiyo kunabainishwa changamoto ya matumizi mabaya ya mamlaka yanayosababisha uvunjifu wa haki za binadamu.
Katika maelezo yake, alirejea oparesheni mbalimbali zilizowahi kufanywa na Serikali kulinda hifadhi na wanyamapori, ikiwemo tokomeza iliyosababisha mauaji ya binadamu.
“Tunapaswa kuangalia namna gani utafanyika uhifadhi kwa kuzingatia haki za binadamu ndiyo msingi wa mjadala tunaotarajia ufanyike,” alisema. |
Wakati Serikali za Tanzania na Kenya zikipitia vipindi vigumu vya mgomo wa wafanyabiashara na maanda | Wakati Serikali za Tanzania na Kenya zikipitia vipindi vigumu vya mgomo wa wafanyabiashara na maandamano ya wananchi, wadau wamependekeza hatua zilizopaswa kuchukuliwa kukabili haraka matukio hayo.
Sambamba na hatua hizo, wanazuoni hao wa biashara na uchumi, wameeleza kilichofanywa katika mataifa hayo kinaonyesha nguvu ya wananchi dhidi ya mamlaka.
Wamesisitiza hatua zilizochukuliwa katika mataifa hayo, zinapaswa kutoa funzo kwamba, wananchi ndiyo wenye maamuzi juu ya hatma ya jambo lolote katika taifa na hivyo ni muhimu washirikishwe.
Kwa upande wa Tanzania, wafanyabiashara walitangaza kugoma kufungua biashara zao Juni 22, mwaka huu na mgomo huo ulianza rasmi Juni 24, katika soko la Kariakoo.
Baada ya maduka katika soko hilo, biashara ziliendelea kufungwa katika mikoa mbalimbali ikiwemo Mbeya, Arusha, Mwanza na sasa hadi Mtwara.
Kwa mujibu wa wafanyabiashara hao, wanagoma kuishinikiza Serikali ibadili mwenendo wa ukusanyaji kodi na ukaguzi wa risiti za mashine ya EFD, ambao wanadai si rafiki kwao.
Katika mwenendo huo, wanasema yanatumika mabavu na vikosi maalumu vya kukagua risiti hizo, lakini hawakuacha suala la utitiri wa kodi katika bidhaa na ukubwa wa ushuru.
Hata hivyo, tangu mgomo ulipoanza, Serikali iliitisha kikao na viongozi wa wafanyabiashara hao na baadaye ilitangaza kusitisha ukaguzi wa risiti hizo za EFD, huku ukiandaliwa utaratibu mzuri wa utekelezaji wa suala hilo katika Soko Kuu la Kimataifa la Kariakoo.
Pamoja na tangazo hilo, bado mgomo uliendelea na mikoa ambayo wafanyabiashara wamefunga maduka yao iliongezeka.
Serikali iliwaita tena wafanyabiashara kukaa mezani na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na kuna madai kuwa maduka yataanza kufunguliwa kuanzia leo.
Kwa upande wa Kenya, muswada wa sheria hiyo unatajwa kuongeza ushuru na kodi katika bidhaa mbalimbali yakiwemo mafuta ya kupikia kwa asilimia 25.
Muswada huo kwa mujibu wa wananchi wa taifa hilo, unakwenda kuongeza gharama za maisha ya Wakenya, huku Serikali ikiendelea kufuja vibaya fedha.
Maandamano hayo yalifikia hatua mbaya zaidi hadi kusababisha vifo vya wananchi 10 na wengine wamejeruhiwa, huku uharibifu mkubwa ukifanyika katika Bunge na maeneo mengine ya umma, ambayo wananchi walivamia.
Kutokana na uharibifu uliofanyika Rais Ruto alilihutubia taifa juzi na kueleza maandamano yanayofanyika yana taswira ya uhalifu na uhaini ndani yake, akitangaza kuruhusu vikosi vya Jeshi la taifa hilo kuzima vurugu zinazoendelea.
Wasomi
Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), alisema sio kwamba wafanyabiashara wanagomea kulipa kodi bali malalamiko yao yamejielekeza katika mazingira rafiki ya kutekeleza wajibu wao huo wa kisheria.
“Ni busara Serikali ingekaa na wafanyabiashara pamoja nina imani suluhu ipo kwenye mazungumzo mezani,” alisema mwanazuoni huyo.
Hata hivyo, alisema mgomo unaleta hasara kwa Serikali, wafanyabiashara na hata mlaji.
“Ukiwasikiliza wafanyabiashara sio kwamba wanapinga kulipa kodi bali wanahitaji ulipaji kodi ulio rafiki kwao na kuboreshewa mazingira ya kulipa kodi hizo,” alieleza.
Kuhusu Kenya, alisema Rais Ruto aache kutia saini muswada huo ili ukose idhini ya kutumika.
“Serikali inapaswa kutosaini muswada huo, ili kupunguza machafuko yanayoendelea au kuyamaliza kabisa. Wananchi wa Kenya wameonesha kutoridhika kwao na mswaada huu,” alisema.
Alisema hilo ni funzo hasa kwa Serikali za Afrika kuheshimu maoni ya wananchi ambao kimsingi ndio wanawaweka madarakani na wenye mamlaka ya kuwaondoa pia.
Maamuzi magumu
Maamuzi magumu ni miongoni mwa mambo muhimu yanayopaswa kufanywa ili kumaliza mgomo wa wafanyabiashara nchini, kama inavyoelezwa na mwanazuoni wa biashara na masoko wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Omari Mbura.
Kwa sabahu mgomo huo unasababishwa na mambo ya kisheria na mengine yasiyo ya kisheria, alisema kwenye yale yanayowezekana Serikali inapaswa kufanya maamuzi kwa kauli moja.
“Kuna maeneo tunayoweza kurekebisha haraka haraka, kusikiliza mteja kuna nafasi kubwa katika shughuli mbalimbali, Serikali iwasikilize na yenye uwezekano wa kuamuliwa haraka ifanywe hivyo hata kama inauma kiasi gani,” alisema.
Katika mgomo huo, alisema anafahamu yapo maeneo ambayo wafanyabiashara nao wana wajibu wa kuyatekeleza, lakini yapo yale wasiyotendewa haki kwayo.
“Kwa mfano Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inafahamu maeneo gani yanayowasumbua wafanyabiashara, hasa kamata kamata sioni kama ustaarabu mzuri,” alisema.
Alisisitiza kuna mambo ambayo Serikali inaweza kuingia moja kwa moja na kutoa tamko la kupata suluhu yake, kisha baadaye itaandaa utaratibu mzuri.
Umuhimu wa kufanyika hayo, alsema unalenga kuepusha hasara inayopatikana sasa katika kipindi ambacho maduka yamefungwa na hakuna kodi inayotozwa wala kukusanywa.
Baada ya kutekelezwa hayo, alisema kila kitakachofanyika, Serikali ihakikisha inazishirikisha jumuiya za wafanyabiashara.
Kuhusu Kenya
Mwanahabari nguli katika habari za takwimu nchini Kenya, Chris Orwa alieleza badala ya kuundwa kodi na ushuru mpya utakaoumiza wananchi, Serikali ilipaswa kutazama kwanza matumizi yake ya ndani.
Kinachoibua hasira zaidi ni kile alichoeleza, Serikali imejiongezea matumizi yasiyo ya lazima, huku ikiwaminya wananchi kupitia muswada huo wa sheria ya fedha uliozaa ushuru mbalimbali.
Kinachopaswa kufanyika kwa mujibu wa mwanahabari huyo, ni Serikali ya Kenya iondoe matumizi yasiyo ya msingi iliyoyaanzisha, kisha fedha zake ndizo zitumike kugharimia mambo mengine.
Miongoni mwa vitu alivyopendekeza kuondolewa kwa kufutwa kabisa ni Ofisi ya mwenza wa Waziri Mkuu, aliyosema imeanzishwa hivi karibuni na huwa na imetengewa bajeti.
“Kuna kitu kimeanzishwa kinaitwa Ofisi ya mwenza wa Waziri Mkuu katika muswada huu inapaswa kutengewa bajeti,” alieleza.
Lingine alisema ni kuondolewa kwa Naibu Mawaziri cheo ambacho awali mahakama ilikiondoa, lakini katika muswada huo kimewekwa na kwamba kitasababisha baraza la mawaziri liwe na watu 50 watakaolipwa Sh1 bilioni ya Kenya kila mwezi.
Badala ya kuweka ushuru kwa wananchi, alisema Serikali ifikirie kuondoa vyeo hivyo ili kupunguza matumizi yake.
Katika muswada huo, Orwa alisema Sh1 bilioni ya Kenya zimepangwa kutumiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na Naibu Rais kununua gari kila mmoja.
“Kwenye muswada huo kuna Sh1 bilioni ya Kenya imetengwa kwa ajili ya Waziri Mkuu na Naibu Rais kupata magari mapya. Hii ni fedha nyingi na inaonekana Serikali inafuja fedha.
Kwa mtazamo wa Profesa Mbura kuhusu yanayoendelea Kenya, alisema ni Serikali kutafuta namna yoyote inayowezekana kuuondoa muswada huo..
“Kilichopo ni kwamba hali imekuwa mbaya kiasi kwamba wananchi wanauchukia muswada wote, yaani kwa sasa huwezi kuwaambia unabadilisha maudhui, Serikali ya Kenya iondoe kabisa muswada husika ili kupunguza ghasia,” alisema. |
Malalamiko ya wafanyabiashara kuhusu utitiri wa kodi, tozo na ushuru wa bidhaa hayakuanza jana, ni k | Malalamiko ya wafanyabiashara kuhusu utitiri wa kodi, tozo na ushuru wa bidhaa hayakuanza jana, ni kilio cha miongo kadhaa katika awamu mbalimbali za Serikali.
Aghalabu malalamiko hayo yanaishia kusikika kupitia wawakilishi wao na ulifika wakati hadi baadhi ya biashara zilishindwa kustahimili hali hiyo zikajifia.
Leo hii, yapo majengo yaliyokuwa na historia kubwa ya biashara, lakini kwa sasa yamesalia kama magofu, yamekosa wapangaji na hata wakazi, yote ni matokeo ya changamoto katika biashara.
Changamoto hizo sio jambo binafsi, zinachagizwa na sheria, kanuni na taratibu ambazo kwa mujibu wa wafanyabiashara zinachagiza ustawi duni wa biashara na hatimaye kufikilisika.
Ukiachana na kasoro za kisheria, matumizi ya nguvu katika usimamizi wa biashara hizo ni tatizo lingine linalowakabili wafanyabiashara katika shughuli zao.
Mara nyingi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetajwa kutumia nguvu katika ukusanyaji wa kodi na inafika hatua hadi ya kufunga biashara za watu, kushinikiza walipe kodi.
Katika utekelezaji wa wajibu huo, kumekuwa na malalamiko ya umbambikizaji kodi hizo na kwa sababu mfanyabiashara hana nguvu ya kisheria anaangukia kwenye mzigo wa deni ambalo hatima yake ni kumfilisi.
Msingi wa hoja yangu hii ni kueleza maoni kadhaa ambayo mara nyingi nimekuwa nikiyasikia kutoka kwa wafanyabiashara, ambayo kwa mujibu wa maelezo yao, ndiyo vikwazo vya biashara zao nchini.
Pamoja na kusikiliza malalamiko ya wafanyabiashara, naelewa wakati mwingine mlalamikaji huvutia kwake, ili kuepuka kuwa na upande nimeyatafakari majibu ya nyakati tofauti yaliyowahi kutolewa na Serikali kuhusu malalamiko hayo.
Yapo yanayotosheleza, lakini yapo yasiyotosheleza na pengine yanaibua maswali mengi zaidi au mtazamo kwamba tegemeo la uchumi wa Serikali ni maumivu kwa wafanyabiashara na wananchi.
Katika mazingira kama haya, ndipo vitu kama migomo ya wafanyabiashara vinapozuka na vikitokea tusiwatishe, tutafute namna ya kuwasikiliza na kutatua wanachodai kuwa tatizo.
Ingawa naeleza hivi si msimamo wangu kuwa mgomo ndiyo njia sahihi ya kudai haki, lakini akili yangu imefika mwisho kuona jambo lingine linaloweza kufanywa kushinikiza upatikanaji wa hicho kinachoitwa haki.
Ukitaka kuona kama kinacholalamikiwa na wafanyabiashara kinagusa maslahi yao, fikiria peke yako kwamba kwa kadri wanavyogoma nao wanapata hasara, kwa sababu hawauzi na kuingiza faida.
Kama mtu anakuwa tayari kuingia hasara ili afanikishe jambo fulani, hapaswi kupuuzwa wala kutishwa, asikilizwe na itatuliwe shida yake na asifichwe kama kuna mkwamo katika ufanikishwaji wa hilo.
Katika siku za hivi karibuni kumetokea mgomo wa wafanyabiashara katika baadhi ya masoko nchini, ambao msingi wake ni malalamiko hayo hayo.
Mbinu za awali zilizotumiwa na Serikali kuzima mgomo huo, kwa maoni yangu hazikuwa sahihi kwani zilihusisha vitisho ndani yake, badala ya busara ya kutafuta namna ya kutatua changamoto zinazolalamikiwa.
Natambua na kupongeza hatua za haraka zilizochukuliwa na Serikali kama kujibu mgomo huo kupitia kikao cha mawaziri wa kisekta na wafanyabiashara, lakini bado kuna juhudi zinahitajika.
Hiki kilichofanyika ni hatua za haraka, wafanyabiashara wanahitaji utatuzi wa kudumu wa matatizo yao, ili ufike wakati wawe huru kufanya shughuli zao.
Yanayohitajika ni mazingira bora na rafiki ya ufanyaji biashara bila kuathiri mitaji ya wafanyabiashara na mapato ya Serikali, hiki ndicho kinacholiliwa.
Natambua umuhimu wa kodi katika maendeleo ya nchi, kadhalika natambua athari za ukwepaji kodi na kuwalea wanaokwepa wajibu huo wa kizalendo na kisheria.
Lakini, Serikali inapaswa kutengeneza mazingira ambayo yataifanya kodi ilipwe kwa hiari na furaha na hatimaye wafanyabiashara kuona ulipaji wa kodi si deni bali ni wajibu wao.
Hayo yote yatafanikiwa kwa kutengeneza mazingira rafiki ya kikodi, uelimishaji wa wananchi kuhusu umuhimu wa kodi, kadhalika kuwaonyesha wananchi miradi iliyotekelezwa kwa kodi hizo.
Ingawa ndiyo uhalisia, lakini ni wananchi wachache watakaoelewa ukiwaambia kodi waliyotozwa imekwenda kulipa watu mishahara, kuwe na utaratibu wa kuonyesha kitu kinachoonekana kwamba kodi imefanikisha hili.
Sambamba na hilo, Serikali ikune kichwa kurasimisha kazi na biashara mbalimbali ili ziwe na vigezo vya kutozwa kodi na hatimaye ipanue wigo wa mapato, ili isilazimike kuwaminya wachache na baadaye wakagoma.
Kuwepo na urafiki baina ya wafanyabiashara na mamlaka zinazowasimamia ili kutengeneza mazingira rahisi na ya kuelewana katika ulipaji wa kodi. Simaanishi ushikaji, nalenga urafiki yaani mnahudumiana huku mnatabasamu.
Wakati tunawatoza kodi wafanyabiashara, tusisahau kuboresha miundombinu wezeshi kwa biashara hizo, ilia aone anachokitoa kimefanikisha lipi na lenye maslahi yepi katika biashara yake.
Isiwe leo unamtoza mfanyabiashara kodi, kesho anashindwa kusafirisha mzigo wa bidhaa kwa sababu ya changamoto ya barabara, ambayo kodi yake ndiyo iliyopaswa kutumika kufanikisha ujenzi wake.
Kwa ujumla wajibu wa utozaji kodi, uende sambamba na haki ya wafanyabiashara kuwekewa miundombinu rafiki ya shughuli zao, hii isiishie kwenye biashara pekee kila eneo. |
Upinzani umeendelea kuishukia kauli ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dk M | Upinzani umeendelea kuishukia kauli ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dk Mohamed Dimwa, aliyetaka Rais Hussein Mwinyi aongezewe muda wa kukaa madarakani kutoka miaka mitano hadi saba.
Msingi wa kauli hiyo ya Dimwa ni kile alichoeleza, sekretarieti ya kamati maalum ya chama hicho imetathmini na kujiridhisha na utendaji wa kiongozi huyo aliyetekeleza kwa zaidi ya asilimia 100 Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa miaka mitatu pekee.
Ukiacha mijadala ya mitandaoni kupinga kauli hiyo, kilichozungumzwa na Dk Dimwa kimepingwa hadi na viongozi waliowahi kukitumikia chama hicho katika nafasi nyeti.
Upinzani wa viongozi hao unatokana na hoja walizoziibua kuwa, kilichozungumzwa na kiongozi huyo kinakwenda kinyume na Katiba ya nchi, ambayo ilipaswa kuheshimiwa.
Ikulu ya Zanzibar nayo imeikana kauli hiyo kwa kusema, Rais Mwinyi ataongoza kwa kufuata utaratibu uliowekwa wa miaka mitano na si vinginevyo.
Wakati wengine wakiibua upinzani huo, Katibu Mkuu wa zamani wa chama hicho, Yusuph Makamba anahoji kwanini watu wanashangazwa na kauli ya Dimwa ilhali kabla yake wapo waliowahi kuzungumza kama hivyo na hakuna aliyeshangaa.
Kinachoelezwa na Makamba, kinarejea kauli mbalimbali za baadhi ya viongozi wa CCM na hata wabunge wakitaka Rais Samia Suluhu Hassan aongezewe muda.
Kauli kama hizo, zilikuwepo pia hata wakati wa uongozi wa Hayati John Magufuli na iliwahi kuzungumzwa pia na Rais wa awamu ya pili, Hayati Ali Hassan Mwinyi.
Msekwa: Ni huzuni
Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Pius Msekwa alisema kauli iliyotolewa kuhusu kumwongezea muda rais huyo, inasikitisha na kuhuzunisha kwa kuwa inachezea Katiba ya nchi.
Kwa mujibu wa Msekwa, Katiba ya nchi si kitu cha kuchezea kama kundi la watu fulani linavyotaka, akisisitiza inapaswa kuheshimiwa.
“Katiba ya nchi si kitu cha kuchezea kama kundi la watu fulani linavyotaka, ni vitu vya kuheshimiwa hadi inapotokea haja ya kuirekebisha kupitia taratibu za zinazopaswa,” alisema.
Alikwenda mbali zaidi na kueleza jaribio kama hilo limewahi kutokea enzi za uongozi wa Salmin Amour, lakini lilizimwa katika vikao vya ndani vya CCM.
Msekwa ambaye pia amewahi kuwa mtendaji mkuu wa chama cha TANU kilichozaa CCM, alisisitiza ni huzuni kauli kama hizo kuendelea kuwepo hata baada ya jaribio la enzi hizo kuzimwa.
“Mimi inanihuzunisha kuona kwamba bado kuna madai ya kuchezea katiba yetu badala ya kuiheshimu,” alieleza.
Hata hivyo, alisema ni imani yake wenye mitazamo kama hiyo watarejea historia na kuona namna ya kujirekebisha.
Ikulu nayo yapinga
Kauli ya Dk Dimwa ilipata upinzani hata kutoka Ofisi ya Rais Ikulu ya Zanzibar, ikieleza kiongozi huyo ataheshimu utaratibu uliopo wa kuongoza kwa miaka mitano.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Charles Hilary, wale wote wenye mawazo tofauti na hayo wanapaswa kufunga mjadala huo.
Katika taarifa hiyo, Ikulu ya Zanzibar ilisisitiza kauli hiyo haina tija wala faida kwa visiwa hivyo na Chama Cha Mapinduzi (CCM), chenye kufuata misingi ya demokrasia.
Si jambo jipya
Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuph Makamba alipoulizwa kuhusu hilo alijibu watu hawapaswi kumshangaa Dk Dimwa, kwa kuwa kauli kama hizo zimewahi kutolewa na viongozi wengi katika awamu mbalimbali za Serikali.
Katika maelezo yake, alimtolea mfano Rais wa awamu ya pili, Hayati Ali Hassan Mwinyi katika moja ya mikutano ya CCM enzi za utawala wa Hayati John Magufuli, alitaka aongezewe muda.
“Kwanini hamjamshangaa Mzee Mwinyi (Hayati) akisema Magufuli aongezewe muda na alisimama kwenye mkutano wa CCM na akasema anafanya kazi vizuri kuliko sisi, hata Ndugai (Job) amewahi kusema,” alihoji.
Mzee Makamba alisema watu kauli kama hizo ni dalili ya viongozi husika kuonyesha kuridhishwa na utendaji wa kiongozi, imekuwa kawaida.
Hata hivyo, Makamba alieleza hata Dk Dimwa hakusema kama kauli yake ni uamuzi, bali aliweka wazi ni maoni anayotarajia kuyapeleka katika vikao vya juu.
“Itakuwa hoja kama vikao vya juu alikosema atalipeleka vitalipitisha, lakini kwa sasa yanabaki kuwa maono yake binafsi na Dimwa si wa kwanza kutoa maoni hayo,” alisema.
Alipoulizwa kuhusu usahihi wa kauli kama hizo, alijibu si ajabu huku akifafanua, “Chanda chema huvikwa pete.”
CCM Zanzibar, bara zakana
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Zanzibar, Khamis Mbetto alisema kilichozungumzwa na Dk Dimwa ni maoni yake binafsi haukuwa msimamo wa chama kama ilivyoaminiwa na wengi.
Maoni hayo ya Dk Dimwa, alisema yametokana na ziara ya sekretarieti ya Kamati Maalum ya chama hicho iliyohusisha kupokea taarifa za utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Baada ya kupokea taarifa hizo, alisema Dk Dimwa ametoa maoni hayo na si msimamo wa wajumbe wa sekretarieti na hata hivyo anayo nafasi ya kuyawasilisha maoni hayo katika vikao vya juu.
“Yalikuwa maoni yake lakini msimamo wa CCM ni kwamba Rais Mwinyi ameapa kutumikia kwa miaka mitano na Katiba ya nchi na chama inasema hivyo,” alisema.
Kuhusu kauli ya Dk Dimwa, alisema ni kama alitereza isipokuwa bado ana nafasi ya kupeleka pendekezo lake hilo katika vikao vya juu ambavyo yeye ni mjumbe.
Kwa sababu suala la kumuongezea kiongozi muda linahusisha mabadiliko ya Katiba ya nchi na chama, alisema kuna michakato mingi kufanikisha hayo.
Kwa mujibu wa Mbetto, kauli ya Dk Dimwa ni kama aliteleza isichukuliwe kuwa ndiyo msimamo wa sekretarieti na chama kwa ujumla.
Kuhusu alichokijibu Makala, Mbetto alisema ni kweli utaratibu wa CCM hufanya maamuzi yake kwa vikao na jambo hilo halikupitia mchakato huo, hivyo ni maoni tu bado haujawa msimamo.
Kwa upande wa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makala naye alisema hakuna jambo hilo, huku akidokeza tayari bajeti ya kugharimia chaguzi zote imeshapangwa, hivyo chaguzi zitafanyika kama kawaida.
Katika mahojiano yake katika kipindi cha Power Breakfast kinachoendeshwa na Kituo cha Redio cha Clouds jijini Dar es Salaam, Makala alisisitiza kilichozungumzwa ni wazo bado si uamuzi.
“Kwa ufupi sana niseme, hilo jambo halipo,” alisema huku akisisitiza CCM inaendeshwa na vikao na kwamba kikao kilichotoa msimamo huo si kile kinachoongozwa na viongozi wa juu.
Alieleza vikao vya chama hicho vinavyofanya maamuzi ni Sekretarieti inayoongozwa na Katibu Mkuu, Kamati Kuu inayoongozwa na Mwenyekiti wa Taifa na Kamati Maalum ya Zanzibar inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti Zanzibar.
Katika vikao vyote hivyo, alisema yeye ni mmoja wa wajumbe na taarifa zote zinazotokana na vikao hivyo zinapaswa kutolewa naye, lakini kuhusu suala hilo hakusikia na halipo kwenye utaratibu wake.
“Nimelisoma kwenye mitandao kama ninyi mlivyosoma. Mimi ndiye Katibu Mwenezi wa CCM, ndiyo msemaji wa CCM, kwa hiyo vikao vyote vya CCM vikimaliza mimi ndiye napaswa kusema, kwa hiyo hilo halipo katika utaratibu wangu,” alisema Makala.
Hata hivyo, alisisitiza kilichozungumzwa katika kikao hicho (alichokisema Dk Dimwa) ni wazo ambalo hata hivyo halijafikishwa katika vikao vikubwa na halikupaswa kuwekwa wazi.
Lakini, msisitizo wa maelezo yake umejikita katika hoja kuwa, bajeti ya mwaka ujao wa fedha, pamoja na mambo mengine fedha imetengwa kwa ajili ya kugharimia chaguzi na hivyo uchaguzi utafanyika kama ilivyopangwa.
“Tumeongelea bajeti hapa, tumeweka hela ya uchaguzi wa Mitaa, tumeweka hela ya uchaguzi mkuu, uchaguzi upo kama kawaida,” alisisitiza. |
Licha ya kusambaa kwa taarifa ya mgomo wa wafanyabiashara katika Soko la Kariakoo utakaoanza leo, ku | Licha ya kusambaa kwa taarifa ya mgomo wa wafanyabiashara katika Soko la Kariakoo utakaoanza leo, kumekuwa na mgongano wa kauli miongoni mwa wafanyabiashara hao.
Mgongano huo unatokana na kauli za viongozi wa wafanyabiashara hao, wanaodai kutohusika na uandaaji wa mgomo huo, huku baadhi ya wafanyabiashara wakisema hawana taarifa za kuwepo kwa mgomo.
Lakini, wengine wanasema wanasubiri kusikia kitakachoamriwa na wengi ili watekeleze, kadhalika wapo wale wenye taarifa za mgomo na wamejiandaa kutekeleza hilo kwa hoja kuwa, wanataka kupaza sauti zao.
Mzizi wa vuguvugu la mgomo huo ni kipeperushi kilichosambaa kutoka sokoni hapo jana na hatimaye katika mitandao ya kijamii kikitoa taarifa ya mgomo wa wafanyabiashara hao kuanzia leo.
Hii si mara ya kwanza wafanyabiashara katika soko hilo kugoma, waliwahi kufanya hivyo Mei mwaka jana, walipofunga maduka wakilalamikia kodi ya forodha bandarini, kodi nyingi wanazotozwa wakiziita chuma ulete.
Mgomo huo uliathiri shughuli za manunuzi hususani kwa wachuuzi wadogo na wakubwa, kutoka ndani na nje ya nchi hadi pale Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipofanya kikao cha pamoja na wafanyabiashara hao na kuunda kamati maalumu ya kushughulikia kero walizokuwa wakilalamikia.
Mwananchi ilifika sokoni hapo jana na kukuta wafanyabiashara mbalimbali wakiendelea na shughuli zao, walipohojiwa mitazamo yao ilijigawa katika makundi matatu.
Wasiosikia kuhusu mgomo
Mwinyimkuu Yusuph ni mmoja wa wafanyabiashara katika soko hilo, alisema hakusikia taarifa yoyote kuhusu mgomo wa wafanyabiashara sokoni hapo.
“Sijasikia chochote kuhusu mgomo, kungekuwa na huo mgomo mwenyekiti angekuwa ameshatuambia nini tunapaswa kufanya hiyo kesho ila hadi sasa hakuna kitu,” alisema.
Kama ilivyo kwa Mwinyimkuu, Zaida Athuman naye hana taarifa rasmi kuhusu mgomo huo, zaidi ya kuona kipeperushi hicho mitandaoni.
Kwa sababu hiyo alisema amebaki kusikiliza na atatekeleza kile kitakachoamriwa kesho.
Baraka Manyanya naye ni wale wale wasio na taarifa, lakini alisema malalamiko ya kukamatwa mara kwa mara na watu wanaodai ni kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilhali hawana utambulisho wowote yamekuwepo.
Taarifa zipo
Wakati wengine wakisema hawa taarifa, baadhi ya wafanyabiashara wanazo taarifa za mgomo huo na Lameck Mbilinyi anayefanya biashara ya vyombo sokoni hapo analithibitisha hilo.
Alisema vipeperushi vya mgomo huo vimepitishwa isipokuwa sababu haijawekwa wazi, huku akiwashari wateja kuhakikisha wanafika sokoni saa nne asubuhi pengine hali itakuwa shwari.
“Jana kila duka lilikuwa linapewa karatasi la tangazo la mgomo kwa sababu watu wanalia kamata kamata imerudi tena, faini ya wasiotoa risiti imeongezeka, hivyo sisi tutafika ofisini kama kawaida ila tutakuwa tunasikilizia kile ambacho kitasemwa na wenzetu,” alisema.
Hata Lilian Kimaro naye anazo taarifa za mgomo, akisisitiza wanafanya hivyo kushinikiza kurahisishwa kwa mazingira ya ufanyaji biashara.
“Wanaosema hawajui ni waongo na wanaogopa kusema ukweli, taarifa zipo kila sehemu,” alisema Lilian.
Alipoulizwa juu ya kuwapo kwa viongozi wao jijini Dodoma katika vikao na viongozi wa Serikali ili kutafuta suluhisho, alisema hayupo na wafanyabiashara kwa sasa, akituhumu kwa kile alichokiita ‘uchawa.’
“Hakuna anachosaidia kwa sasa zaidi ya kuwa chawa kwa viongozi wakati sisi huku tunahangaika na hali ngumu ya biashara,” alisema na kuongeza “Si kugoma tu hadi kuandamana.”
Mzizi mwingine wa kugoma kwao ni kile kilichoelezwa na Lauren Massawe anayefanya biashara ya vitenge sokoni hapo, kumekuwa na kukamatwa kwa madai ya kutotoa risiti, hivyo wanagoma kufikisha malalamiko yao.
Hata hivyo, alieleza kugoma huko pia, kunalenga kushinikiza kupata mrejesho wa malalamiko yao ya mwaka jana.
“Kumekuwa na ukamati kwa wateja kupitia TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) na malalamiko yetu ya mwaka jana hayajafanyiwa kazi kwa sababu hatujapata mrejesho hadi leo na hatujui mamuzi yaliyotolewa ni yapi,” alisema.
Mkuu wa mkoa aibuka
Kutokana na taarifa hizo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila alisema tayari baadhi ya changamoto za wafanyabiashara katika soko hilo zilianza kufanyiwa kazi Wizara ya Fedha, Viwanda na Biashara, Halmashauli za jiji hilo na sekta nyingine muhimu zilizokuwa zinalalamikiwa.
TPSF
Mkurugenzi wa TPSF, Raphael Maganga kupitia taarifa yake kwa umma aliwataka wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao wakati majadiliano ya muswada wa fedha unaendelea bungeni.
“Tunapenda kusisitiza wafanyabiashara kuendelea kuitumia mifumo yao rasmi yaani (vyama vya biashara) kupeleka hoja zao, kulipa kodi zao stahiki na kwa wakati ili kuepuka na usumbufu unaoweza kujitokeza.
Tunatambua kodi hizi zinafaa kuwa za haki, zenye usawa na sio zenye dhuluma kwa pande zote ili watanzania wengi wachangie kwenye maendeleo ya taifa letu,” ilieleza taarifa hiyo.
Katika taarifa hiyo, alitaka zisisambazwe habari zisizo sahihi ili kuepuka taharuki, huku akizita taasisi za Serikali kuhakikisha zinatekeleza majukumu yao kwa weledi na kutatua kero za wafanyabishara kwenye maeneo yao husika.
Polisi
Hata hivyo, Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, David Misime limewahakikishia ulinzi wafanyabiashara wa soko hilo watakaotaka kuendelea na shughuli zao pamoja na wanunuzi watakaofika sokoni huku likiwatafuta waliosambaza tangazo hilo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabisahara Tanzania (JWT), Hamis Livembe alisema mgomo huo hauna baraka za viongozi, kwa kuwa hata alipowasiliana na wasimamizi wa wafanyabiashara sokoni hapo hawakuwa na taarifa.
“Mgomo hauna baraka za viongozi, sisi pia tumesikia uwepo wake kama ninyi mlivyosikia, tumeona katika mitandao ya kijamii vipeperushi na katika baadhi ya makundi yetu mitandaoni lakini tulipojaribu kuwasiliana na viongozi wa wafanyabiashara mikoa, wilaya na hapo Kariakoo nao walikuwa hawajui,” alisema Livembe. |
Licha ya sekta ya kilimo kuwa msingi wa ajira za Watanzania lukuki, wakulima wengi nchini wanakosa m | Licha ya sekta ya kilimo kuwa msingi wa ajira za Watanzania lukuki, wakulima wengi nchini wanakosa maarifa sahihi ya namna ya kuienenda shughuli hiyo.
Kukosekana kwa maarifa hayo miongoni mwa wakulima wengi nchini, kunasababisha kilimo kifanyike kwa mazoea na hatimaye kukosa tija katika uzalishaji.
Asilimia 75 ya Watanzania wamejiajiri katika shughuli za kilimo na sekta hiyo huchangia nusu ya pato la taifa, kwa mujibu wa takwimu za Serikali.
Lakini, kutokana na idadi ya Watanzania waliojiajiri katika sekta ya kilimo, sekta hiyo ilipaswa kuchangia robo tatu au zaidi katika pato la taifa.
Maarifa duni ya utekelezaji wa shughuli za kilimo ndiyo yanayosababisha kukosekana tija na hivyo sekta hiyo iendelee kuwa na mchango mdogo katika pato la taifa.
Ili kuiinua sekta hiyo na iwe na mchango tarajiwa kama ilivyo katika malengo ya Serikali, shamba darasa ni jambo muhimu kuzingatiwa.
Shamba darasa linasaidia wakulima kufahamu teknologia na mbinu mpya za kilimo, ikiwemo matumizi ya matandazo, mbegu zinazostahimili mabadiliko ya tabianchi, viwatilifu asilia (mwarobaini, pilipili, vitunguu swaumu n.k) samadi, mboji na nyinginezo.
Kupitia shamba darasa mkulima anajufunza aina mpya za mbegu za mazao zinazostahimili mabadiliko tabianchi, jinsi ya ulimaji wake, huduma na utunzaji.
Mfano mtu anayetaka kulima Nyanya chungu kupitia shamba shamba darasa anashauriwa aina ya mbegu bora, mbinu mbali mbali za upandaji, umwagiliaji, matumizi ya viwatilifu asilia zidi ya visumbufu vya mazao, pamoja usimamizi wa mazao yake.
Taasisi Isiyo ya Kiserikali ya TWINS AGROVET, ni kielelezo cha umuhimu wa shamba darasa katika kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo.
Taasisi hiyo hadi sasa, imenufaisha jumla ya vikundi 212 vya wakulima wa mazao mbalimbali yakiwemo maharage na mboga mkoani Simiyu, baada ya kuvijengea uwezo juu ya namna ya kutumia mbinu za kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi.
Mbinu hizo za kilimo kwa mujibu wa wakulima walionufaika na mradi wa kuwajengea uwezo katika kanuni bora za kilimo unaotekelezwa na taasisi hiyo kwa awamu ya tatu zimewawezesha kuongeza mavuno.
Kupitia mradi huo unaotekelezwa katika Wilaya zote za Mkoa wa Simiyu, wakulima hao wamesema wanashuhudia kupungua kwa gharama za kilimo na ongezeko la mavuno katika mazao yao.
Salawa Mahembe ni miongoni mwa wakulima hao, amesema kwa sasa ana uwezo wa kupanda zao zaidi ya moja katika shamba moja, kadhalika anatumia viuatilifu vya asili kudhibiti wadudu.
Mbinu wanazotumia, amesema ni dawa wanazozitengeneza wenyewe, ambazo ni Lantana, Mwarobaini, Matulatula na Pilipili.
Kupitia mradi huo, ameeleza amejifunza namna nzuri ya uandaaji wa mazao katika mbinu zitakazokabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Miongoni mwa mbinu hizo, amesema ni uandaaji wa mbolea ya Mboji inayohusisha kinyesi cha ng’ombe, badala ya kwenda kununua dukani.
Mkulima mwingine anayejishughulisha na kilimo cha maharage, Mlya Masunga amesema baada ya elimu hiyo katika shamba la mfano la robo ekari wamevuna debe saba.
Amesema mavuno hayo ni mara sita zaidi ya yale waliyokuwa wakiyapata kabla ya elimu hiyo, akisema katika shamba lenye ukubwa huo wangevuna debe moja.
“Kwa mradi huu mtu atapata mazao mengi na kumkomboa kimaisha. Kila mtu atapata nafasi nzuri ya kufanya kilimo cha kisasa na kuepuka athari za mabadiliko ya tabianchi,” amesema.
Ameishukuru TWINS AGROVET kwa kuwapa elimu iliyowawezesha kufanya kilimo cha kisasa bila kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi.
“Tunawashukuru na tunawaomba wengine wajiunge na huu mradi wa maharage ili wanufaike na elimu katika msimu ujao wa kilimo,” amesema mkulima huyo. |
Hatma ya maumivu au unafuu wa maisha kwa wananchi, itaamuliwa na wabunge wiki hii wanapokwenda kupit | Hatma ya maumivu au unafuu wa maisha kwa wananchi, itaamuliwa na wabunge wiki hii wanapokwenda kupitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/25.
Sambamba na hilo, wiki hii ndiyo itakayoamua hatma ya tuhuma za kudharau mamlaka ya Spika na Bunge zinazomkabili Mbunge wa Kisesa (CCM), Luhaga Mpina.
Wiki mbili zilizopita Serikali ilipendekeza kukusanya na kutumia Sh49.3 trilioni ikiwa ni bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25, huku hoja mbalimbali zikiibuliwa na wabunge wakigusa maeneo yanayoumiza wananchi.
Miongoni mwa hoja hizo zilizoibuliwa ipo inayohusu sheria mpya ya kodi ya Sh382 kwa kilo moja ya gesi ya magari, ambayo baadhi ya wabunge wameonyesha kuipinga.
Sakata la bei ya sukari kupanda kila mwaka, kikokotoo, madeni ya Serikali kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, watu kujificha kwenye kauli ya ‘mama anaupiga mwingi’ na matumizi ya malipo kwa mfumo wa kidigitali ni hoja nyingine zilizoibuliwa.
Kama hiyo haitoshi, ugumu wa upatikaji dola ya Marekani na jinsi ya kupunguza matumizi ya fedha hizo, madeni ya wakandarasi wa ndani na nje ni baadhi ya hoja nyingine.
Zote hizo zinawasubiri Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo wazijibu kisha upitishaji wa bajeti hiyo uendelee.
Baada ya kuhitimisha wabunge watapiga kura kwa utaratibu wa kuitwa mbunge mmoja mmoja kwa jina na kuulizwa iwapo anaunga mkono na kisha kuhesabiwa kwa kura zitazotoa uamuzi kuhusu bajeti hiyo.
Wanazuoni
Akizungumza na Mwananchi jana, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Lutengano Mwinuka alisema wabunge wengi wametimiza wajibu wao kwa kutetea wananchi wao na majimbo yao katika mjadala wa bajeti.
Alisema wamegusa maeneo ambayo ni changamoto kwa wananchi ikiwemo barabara za vijijini ambapo vipaumbele vya kuzijenga vipo lakini kutokana na uhaba wa fedha wakukidhi mahitaji yote.
Alisema katika mijadala ya bajeti hiyo, pia wameona wabunge wengi wakijaribu kuzungumzia umuhimu wa baadhi ya mabadiliko ya kisera yavyoweza kulinda viwanda vya ndani ikiwemo eneo la sukari.
“Lakini ni dhahiri Serikali haiwezi kuacha wadau wake, imefafanuliwa mara kadhaa na Waziri wa Kilimo kuwa walaji na viwanda vinalindwa. Takwa la Serikali halipishani sana na mahitaji ya wabunge sema tu uhaba wa raslimali ambayo ni changamoto ya kila mwaka,”alisema Mwinuka ambaye ni mchumi kitaaluma.
Najim Hamad mkazi wa Kimara Dar es Salaam, alieleza kilichobaki ni uamuzi wa kupitisha au kutopitisha kwa kuwa hoja zilizoibuliwa zimejitosheleza.
Hamad anayejishughulisha na udereva wa Taksi Mtandao, alisema amesikia maoni na hoja za wabunge kuhusu kodi kwenye gesi zinazotumika katika magari na kwamba ameridhishwa nayo.
Lakini, alisema kinachosubiriwa ni maamuzi ya kuipitisha sheria hiyo au kuibatilisha kutokana na hoja zilizoibuliwa.
“Wabunge siwadai chochote, wameeleza vizuri ile inatuumiza hasa sisi tunaofanya biashara hizi (taksi mtandao), tunasubiri maamuzi na nayasubiri kwa hamu,” alisema.
Hoja ya kubana matumizi ya Serikali ndiyo maamuzi yanayosubiriwa na Delta Maziku kutoka bungeni wakati wa upitishaji wa bajeti hiyo.
“Ni maamuzi haswa kwa sababu yale yote yaliyosemwa na wabunge yanakwenda kuamuliwa sasa ndani ya bajeti hiyo,” alisema.
Mpina naye ataijua hatma yake
Leo ndio itakuwa ni siku ya kuwasilishwa kwa Kamati ya Bunge ya Haki Kinga na Maadili na Madaraka ya Bunge kuwasilisha taarifa yake kuhusu tuhuma zinazomkabili Mpina za kudharau mamlaka ya Spika na Bunge.
Pia kamati hiyo itawasilisha taarifa ya walichokiona katika ushahidi wa Mpina kuhusu tuhuma alizozitoa kuwa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema uongo bungeni wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Fedha Juni 4, mwaka 2024.
Taarifa hiyo, inatokana na uamuzi wa kumpeleka katika kamati hiyo uliotolewa Juni 18, 2024 na Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson ambaye alisema kupeleka ushahidi alioamuagiza kwenye vyombo vya habari ni kudharau mamlaka ya Spika.
Dk Tulia alisema pia kitendo hicho ni kuingilia mwenendo wa Bunge na kushusha hadhi na heshima ya Bunge.
Pia, Spika amezipeleka kwenye kamati hiyo nyaraka za ushahidi wa Mpina dhidi ya Waziri wa Kilimo Bashe kwamba amelidanganya Bunge kuhusu utoaji wa vibali vya kuingiza sukari nchini.
Dk Tulia alisema ni dhahiri kitendo cha Mpina kuwasilisha nyaraka za ushahidi kwa Spika na wakati huo huo kwenda kuzungumza kwenye vyombo vya habari kuhusu maudhui ya nyaraka hizo ni kitendo cha utovu wa nidhamu kwa Bunge na Spika.
“Kifungu cha 26 (d) cha sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge, sura 296 kinazuia kitendo cha kumkosea heshima Spika.
“Kifungo cha 26 (e) kinazuia vitendo vya dharau kwa mwenendo wa shughuli za Bunge, aidha kifungu cha 34, kifungu kidogo cha kwanza (g) kinazuia kuchapisha kwa umma taarifa zilizoandaliwa mahususi kwa ajili ya kuwasilishwa bungeni pasipo kupata kibali cha Bunge na kabla ya taarifa hizo kuwekwa mezani.
“Kitendo cha Mpina kinakwenda kinyume na kifungu cha 29 (d na e) na kifungu cha 34, kifungu kidogo cha kwanza (g) vya sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge sura 296.
Akizungumzia adhabu hizo, Wakili Elias Machibya alisema kupewa adhabu ya kufungiwa kuna waathiri pia wapiga kura kwa kukosa uwakilishi pindi mbunge huyo anapozuia kuingia katika vikao vya Bunge.
“Wananchi wakikosa uwakilishi ina maana wanakosa sauti ya kuwasemea. Lakini mtu ambaye ni mbunge anatakiwa kuwa na tabia ambazo ni kielelezo kwa jamii kwa sababu mbunge ni kiongozi wa kitaifa,”alisema.
Alisema hivyo inapasa mbunge kujitunza kwa kujua kuwa anadhama sio tu kwa wapiga kura wake, bali ya Bunge pia.
“Kanuni za Bunge zinachukua mkondo wake kwa mtu yoyote akionyesha tabia isiyofaa ili kulinda hadhi na heshima ya Bunge…Kwa Spika asiposimamia vizuri sheria anaweza kufanya Bunge kushusha hadhi kwa jamii,”alisema.
Machbya alisema hakuna namna ya kulegeza adhabu hizo kwa kwa sababu watashusha hadhi ya Bunge, hivyo ni jukumu la wabunge kukaa sawa kimaadili ili kulinda hadhi na heshima ya Bunge kwa ajili ya maslahi ya Taifa na wapiga kura wake.
Waliowahi kubanwa na kamati hiyo
Baadhi ya wabunge ambao waliwahi kukutana na kibano cha kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge ni Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Saed Kubenea (Ubungo), James Ole Miliya (Simanjiro) na Suzan Lyimo na Anatropia (Viti Maalumu) wote walikuwa Chadema.
Wengine ni Tundu Lissu (Singida Mashariki), Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), Godbless Lema (Arusha Mjini), Conchesta Rwamlaza (Viti Maalum), Jesca Kishoa (Viti Maalum), pia walitokana na Chadema.
Kwa upande wa CCM Josephat Gwajima (Kawe) na Jerry Silaa (Ukonga), Stephen Masele (aliyekuwa mbunge wa Shinyanga Mjini).
Halima Mdee na Ester Bulaya (viti maalumu) ndio waliowahi kupewa adhabu kubwa ya kufungiwa kutohudhuria Bunge mikutano 4 (mwaka 1) baada ya mapendekezo ya Kamati ya Kudumu ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.
Wabunge hao walituhumiwa kudharau mamlaka ya spika kwa kukaidi maelekezo yake ya kuwataka watulie ili Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde aliyepewa nafasi ya kuzungumza aendelee.
Hata hivyo, kamati hiyo iliwahi kutoa msamaha kwa aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kwa kosa la kudharau mamlaka ya Spika ikiwemo kupiga kelele bungeni na kutupa karatasi ovyo.
Iwapo Mpina atakumbana na aina yoyote ya kibano kutoka kwa kamati hiyo, kuna uwezekano akabanwa pia na chama chake ambacho awali Kamati ya Maadili ya CCM Wilaya ya Meatu.
Atakapohukumiwa kwa kudharau mamlaka ya Spika na kulidharau bunge, maana yake amezidharau mamlaka ambazo CCM inaziheshimu na hivyo dharau hizo zitaamua kuiadhibiwa ndani ya chama chake.
Adhabu zinazowezekana kwa mbunge huyo, kwa mujibu wa Kanuni za Maadili za chama hicho ni kupewa karipio, kuonywa na asipojirekebisha ndani ya kipindi cha adhabu atafukuzwa uanachama.
MWISH0
Wakati Jeshi la Polisi likiendelea kumshikilia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk Yahaya Nawanda, wataalamu wa sheria wametaja mazingira yanayowezesha kuendelea kushikiliwa kwake, huku wengine wakisema anastahili dhamana.
Dk Nawanda alikamatwa na Polisi Juni 13, mwaka huu, kwa tuhuma za kumwingilia kinyume na maumbile mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza, ndani ya gari lake.
Matarajio ya wengi ilikuwa ni kuona ama mtuhumiwa huyo anapelekwa mahakamani au anapewa dhamana baada ya saa 24 tangu alivyokamatwa na jeshi hilo kama inavyoelekezwa katika Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai sura ya 20.
Kifungu cha 32 cha sheria hiyo kinasema, “mtu yeyote akikamatwa na jeshi la polisi akiwa mikononi mwao isipokuwa kwa makosa ambayo adhabu yake ni kifo au makosa yaliyo na mazingira magumu, haraka iwezekanavyo anapaswa kufikishwa mahakamani kwa muda usiozidi saa 24, vinginevyo apewe dhamana kwa masharti yatakayokubaliwa.”
Anaendelea kushikiliwa
Licha ya sheria kueleza hivyo, Mwananchi jana lilizungumza na Msemaji wa jeshi hilo, David Misime juu ya kinachoendelea kuhusu Dk Nawanda, alisema: “Subirini.”
Alipoulizwa hadi lini, Misime alisema katika taarifa iliyotolewa awali na jeshi hilo ilielezwa uchunguzi ukiwa tayari taarifa zaidi zitatolewa.
Mwananchi lilipotaka kujua ziadi ni kwa nini wanaendelea kumshikilia zaidi ya saa 24, Misime alisema kuna mazingira yanaweza kuwafanya kuendelea kumshikilia kwa mujibu wa sheria.
Alipaswa apewe dhamana
Akizungumzia hilo, Wakili wa kujitegemea, Jebra Kambole alisema kisheria polisi wanapomtia nguvuni mtuhumiwa, wanapaswa kumpeleka mahakamani ndani ya muda usiozidi saa 24.
Hata hivyo, sharti la kumpeleka mtuhumiwa mahakamani ndani ya muda huo, alisema linatokana na aina na mazingira ya kesi husika.
Mathalan, kwa kesi zilizokuwa katika mazingira magumu zikiwemo zile ambazo adhabu zake ni kifungo cha maisha au kunyongwa, alieleza polisi wanaweza wasimpeleke mtuhumiwa mahakamani ndani ya muda huo.
Lakini, alisema hawapaswi kuendelea kubaki naye, badala yake anastahili kupewa dhamana huku mambo mengine kama kukamilisha ushahidi yakiendelea.
Msingi wa ufafanuzi wa Wakili Kambole ni kifungu cha 32 cha Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20.
Kifungu hicho kinaeleza: “mtu yeyote akikamatwa na jeshi la polisi akiwa mikononi mwao isipokuwa kwa makosa yaliyo na mazingira magumu, haraka iwezekanavyo anapaswa kufikishwa mahakamani kwa muda usiozidi saa 24.”
Aliyafafanua makosa yaliyo katika mazingira magumu ni yale ambayo adhabu zake ni ama kifungu cha maisha jela au kunyongwa na aghalabu ni kosa linalohusisha mauaji ya zaidi ya mtu mmoja.
Hata hivyo, alisema katika mazingira ya makosa ya namna hiyo bado polisi hawapaswi kubaki na mtuhumiwa mahabusu, anastahili kupewa dhamana.
“Sio sawa kumshikilia kwa zaidi ya muda huo ni vizuri wakampa dhamana au wakampeleka mahakamani, hata kama upelelezi haujakamilika,” alisema.
Kwa mujibu wa Kambole, sababu za masharti hayo ni uhalisia wa mazingira ya vituo vya polisi kutokuwa na miundombinu wezeshi ya kumwezesha binadamu kukaa kwa zaidi ya saa 24.
Anawezaje kukosa dhamana?
Hata kama kosa linadhaminika kwa mujibu wa sheria, yapo mazingira yanayosababisha mtuhumiwa aendelee kushikiliwa na kunyimwa dhamana, kama inavyofafanuliwa na Dk Iddi Mandi mhadhiri wa masuala ya sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Kwa mujibu wa Dk Mandi, Polisi wanaruhusiwa kuendelea kumshikilia mtuhumiwa kwa zaidi ya saa 24 na bila kumpa dhamana iwapo itabainika kupewa kwake dhamana kunaweza kuathiri upelelezi.
“Ikibainika mtuhumiwa iwapo atapewa dhamana ana uwezo au nguvu ya kwenda kuharibu ushahidi, katika mazingira hayo huwa anaendelea kushikiliwa hata kama kosa lake linadhaminika,” alisema.
Mazingira mengine yanayosababisha mtuhumiwa kuendelea kushikiliwa, alieleza ni iwapo itabainika kuachiwa kwake kunaweza kuathiri usalama wake.
“Hii ni katika mazingira ambayo, pengine mtuhumiwa akiachiwa anaweza kupigwa na wananchi wenye hasira kali au kudhuliwa kwa namna yoyote, katika kumlinda inabidi abaki ndani,” alifafanua.
Dk Mandi alisema mazingira mengine yanayoweza kumwacha mtuhumiwa ndani ni kama kosa lake halidhaminiki, ikiwemo mauaji ya kukusudia, uhaini na utakatishaji fedha. |
Siku tatu baada ya kupatikana mwili wa mtoto, Asimwe Novath (2) mwenye ualbino, hatimaye Jeshi la Po | Siku tatu baada ya kupatikana mwili wa mtoto, Asimwe Novath (2) mwenye ualbino, hatimaye Jeshi la Polisi limewakamata watu tisa wanaodaiwa kuhusika na mauaji yake, akiwemo Paroko Msaidizi na Baba mzazi wa mtoto huyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo, tisa hao wamekamatwa wakiwa na viungo mbalimbali vinavyodaiwa kuwa vya mtoto huyo, walivyovihifadhi katika vifungashio vya plastiki tayari kutafuta wateja.
Pamoja na hatua hiyo, wadau wa utetezi wa haki za binadamu wamesema hawakuridhishwa na mwitikio wa mamlaka zinazohusika katika kushughulikia taarifa za awali za kupotea kwa mtoto huyo.
Mwili wa Asimwe ulipatikana Juni 17, mwaka huu kwenye kalavati katika barabara ya Luhanga wilayani Muleba mkoani Kagera, huku baadhi ya viungo vikiwa vimenyofolewa.
Awali, Asimwe aliporwa mikononi mwa mama yake Mei 30, mwaka huu, nyumbani kwao Muleba na siku 19 baafaye ulipatikana mwili wake na juzi ulizikwa.
Tisa waliokamatwa
Taarifa rasmi ya kukamatwa kwa watu hao, ilitolewa jana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime, akisema kati ya tisa hao waliokamatwa yumo Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bugandika wilayani Misenyi katika Mkoa wa Kagera na baba mzazi wa Asimwe, Novart Venant.
Kupitia taarifa hiyo, Misime alisema watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na viungo vinavyodhaniwa ni vya Asimwe, walivyovihifadhi katika vifungashio vya plastiki wakitafuta mteja.
Alieleza watuhumiwa hao wamekamatwa katika kipindi cha kuanzia Mei 31 msako ulipoanza hadi usiku wa kuamkia Juni 19, mwaka huu.
Aliwataja wengine waliokamatwa ni Desideli Evarist ambaye ni mganga wa jadi mkazi wa Nyakahama, Dastan Kaiza mkazi wa Bushagara, Faswiru Athuman mkazi wa Nyakahama na Gozibert Alkadi mkazi wa Nyakahama Kamachumu.
Kadhalika, wamo Rwenyagira Burkadi mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Ramadhani Selestine mkazi wa Kamachumu na Nurduni Hamada mkazi wa Kamachumu.
“Elipidius Rwegoshora Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bugandika ndiye anayedaiwa kumfuata na kumshawishi Baba mzazi wa mtoto ili wafanye biashara ya viungo vya binadamu.
“Pia anatuhumiwa kuwa ndiye aliyemtafuta mganga wa jadi na kulipia gharama zote za uganga,” inaeleza taarifa hiyo.
Kupitia taarifa hiyo, Misime alisema watuhumiwa waliokamatwa walieleza jinsi walivyoshiriki katika tukio hilo kwa kushirikiana na baba mzazi wa mtoto.
“Jeshi la Polisi linatoa onyo kali kwa watu wanaoendekeza imani za kishirikina ikiwemo kupiga ramli chonganishi wakiaminishana kwamba wanaweza kupata utajiri kwa njia za kishirikina kuacha tabia hizo,” alisema.
Taarifa hiyo imetaka wananchi waache kudanganyana kwamba kuna utajiri unaopatikana kwa kumiliki viungo vya binadamu mwenye ualbino kwa kuwa si kweli.
“Kama ingekuwa hivyo familia zenye watoto au ndugu wenye ualbino wangekuwa na utajiri mkubwa lakini badala yake tunaona wakiishi maisha ya kawaida kama sisi wengine,” amesema.
Watetezi wadai kutoridhishwa
Katika taarifa yao ya pamoja Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), walieleza kulaani tukio hilo.
Pamoja na kulaani, mashirika hayo ya utetezi wa haki za binadamu, yalieleza kutoridhishwa na mwitikio wa mamlaka husika katika kushughulikia taarifa za awali za kupotea kwa mtoto huyo.
“Mwitikio huo ni katika kutoa taarifa kwa umma kujulisha jitihada zilizochukuliwa punde baada ya taarifa ya kupotea kwa mtoto huyo,” alisema Fulgence Massawe kaimu mkurugenzi mtendaji wa LHRC.
Alieleza hata taarifa ya kuwatafuta waliohusika na tukio hilo haikutolewa wakati huo, jambo ambalo kwa mujibu wa Massawe, linaongeza hofu katika usalama wa jamii ya watu wenye ualbino.
Tukio hilo, alisema linapaswa kuikumbusha Serikali na mamlaka zote juu ya umuhimu wa juhudi za pamoja kukabiliana na unyanyasaji dhidi ya wenye ualbino.
Katika taarifa hiyo, mashirika hayo yaliweka wazi kuwa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD), iliisikitikia Tanzania kwa kukosa utayari wa kufutilia maombi matatu tyaliyowasilishwa kwenye kamati hiyo.
Maombi hayo kwa mujibu wa Massawe ni kutowajibika kwa Tanzania katika ukataji wa viungo vya watu wenye ualbino.
“Kushindwa kulaani na kuchunguza mashambilizi dhidi ya watu hao, kunaweza kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa wajibu wa Serikali wa kuwalinda watu wenye ulemavu,” alisema Massawe.
Kutokana na hayo, mashirika hayo yalitoa wito kwa Jeshi la Polisi kuchunguza tukio hilo na kuwakamata wahusika wote, wakiwemo walioratibu uuaji na utekaji na watumiaji wa viungo hivyo.
“Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu waweke mkakati madhubuti wa kuwatambua na kusimamia ustawi wa watu wenye ualbino katika maeneo yote nchini,” alisema Remmy Lema, ofisa mipango wa THRDC.
Alilitaka bunge kutumia kipindi cha bajeti kujadili na kuweka fungu maalum ili kuimarisha mifumo ya ulinzi wa watu wenye ualbino katika ngazi zote.
Aliitaka jamii kuendelea kuwaripoti watu wote wanaojihusisha na vitendo vya ukatili dhidi ya wenye ualbino ili vyombo vya ulinzi na usalama vichukue hatua.
“Jamii iachane na imani potofu ya matumizi ya viungo vyua watu kuvihusisha na utajiri au kujipatia mamlaka katika ngazi mbalimbali. Wanajamii wasimame kupinga vitendo hivi,” alisema Remmy.
Waziri
Awali, kabla ya taarifa ya Polisi Mwananchi ilizungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alisema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha wanakamata mtandao wote wa wanaohusika na vitendo hivyo.
Msingi wa kufanya hivyo ni kile alichofafanua kuwa, wanachokitaka ni kung’oa mizizi ya wahusika wa vitendo vya ukatili dhidi ya wenyewe ualbino.
Kuhusu kutoa taarifa mapema kwa umma, alisema isingewezekana kwa hofu ya kuharibu uchunguzi akisema, “hatuwezi kuanika silaha zetu hadharani wakati maadui zetu bado wako nje.”
Lakini, alisema kuna umuhimu wa kuwajulisha wananchi ili wafahamu juu ya hatua zilizofikiwa ili nao watoe msaada unaowezekana kukabiliana na hali hiyo.
“Bahati mbaya kuokoa maisha ya mtoto hatukufanikiwa, lakini la kuwapata wahusika tumefanikiwa. Sio kwamba tunabahatisha, wamepatikana na vidhibiti,” alifafanua.
Baadaa ya kuwakamata, Masauni alisema kinachofanyika sasa ni kufukua mizizi ya wahusika wote wa vitendo vya ukatili dhidi ya wenye ualbino.
“Hatapona mtu katika hili, yaani hakuna mtu hata mmoja aliyehusika na udhalimu wa huyu mtoto malaika wa Mungu atakayepona na tumefikia pazuri sana.
“Nakueleza haya kwa sababu najiamini na hii inakuwa fundisho kwa wengine wanaofikiria kufanya udhalimu huo watakwisha,” alisema Waziri huyo.
Kwa sasa, alisema jeshi la polisi lipo imara kuhakikisha linakomesha kila aina ya uhalifu, akisisitiza hakuna mhalifu ambaye hatakamatwa.
“Naliweka wazi hilo ili wananchi wajue na wawe na imani na Serikali yao kwamba Jeshi la Polisi lina motisha kwa sasa na limejengewa uwezo sidhani kama kuna shida kwao, askari wetu wanavitendea kazi vya kutosha na wana molari ya kutosha,” alisema. |
Michakato ya kuelekea uchaguzi imehusishwa kama moja ya sababu za mauwaji ya watu wenye ualbino, huk | Michakato ya kuelekea uchaguzi imehusishwa kama moja ya sababu za mauwaji ya watu wenye ualbino, huku wadau wakitaja kasoro zilizopo katika kuyakabili matukio hayo.
Miongoni mwa kasoro zilizobainishwa na wadau hao ni uwepo wa mianya ya uholela katika shughuli za uganga wa jadi na kukosekana mrejesho wa hatua zinazochukuliwa dhidi ya wanaohusika.
Wadau hao wamerusha lawama kwa wananchi pia, wakisema baadhi yao wanawajua wanaohusika, lakini wanaendelea kuwaficha kwa hofu ya kusimama mahakamani kutoa ushahidi.
Hata hivyo, Jeshi la Polisi limesema pamoja na hatua kali za kisheria, litaendelea kutoa elimu kwa jamii ili iondokane na kile lilichokiita kudanganyana kuwa, kuna mafanikio katika viungo vya binadamu mwenzako.
Mzizi wa kuibuliwa kwa hoja hizo za wadau ni matukio ya hivi karibuni, likiwemo lililoondoa uhai wa mtoto Asimwe Novath (2) mwenye ualbino, ambaye Mei 30, mwaka huu alinyakuliwa mikononi mwa mama yake.
Tangu aliponyakuliwa mtoto huyo alitafutwa bila mafanikio, hadi Juni 17, mwaka huu mwili wake ulipopatikana ukiwa umefungwa katika mfuko wa sandarusi, huku baadhi ya viungo vikiwa vimenyofolewa.
Tukio hilo lilitanguliwa na lililotokea Mei 4, mwaka huu, Katoro mkoani Geita, mtoto Julius Kazungu (10) alinusurika kufa baada ya kujeruhiwa na kitu chenye ncha kali kichwani na mikononi.
Haya si matukio ya kwanza, kumekuwa na historia ya kutokea kwa mauwaji au kushambuliwa kwa watu wenye ualbino hasa katika kipindi unapokaribia uchaguzi.
Hilo linathibitishwa na ripoti ya mwaka 2013 ya Shirika la Under The Same Sun, iliyobainisha watu 73 wenye ualbino waliuawa kwa kipindi cha miaka sita hasa nyakati za kuelekea uchaguzi.
Wadau wataja kasoro
Akizungumza na Mwananchi jana Mratibu wa kitaifa wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika (WiLDAF), Anna Kulaya alibainisha maeneo yenye kasoro katika kuvidhibiti vitendo hivyo.
Alieleza kwa kuwa waganga wa jadi ndiyo wanaotajwa kupiga ramli chonganishi, inashindikanaje kuwachunguza kwa kinaili kupata undani wa shughuli zao.
Sambamba na hilo, alisema anayetoa vibali vya waganga hao kufanya kazi, anajiridhisha na mambo yepi na anafuatilia vipi mwenendo wa kazi za uganga huo.
Alieleza kujirudia kwa matukio hayo, kunaashiria mamlaka zinazohusika zimeshindwa kuwalinda watoto na watu wazima wenye ualbino.
Alikwenda mbali zaidi na kufafanua matukio hayo yanahusishwa na michakato ya uchaguzi, akisema inashindikanaje kujenga utamaduni wa kuchukia mauwaji ya wenye ualbino.
“Kwanini tusitengeneze utamaduni wa kutovumilia vitendo vya mauwaji ya albino leo hii pengine visingekuwepo,” alisema Anna.
Ukiachana na mamlaka, Anna alitaja kasoro zilizopo kwa wananchi na hivyo kusababisha kuendelea kwa matukio hayo, ikiwemo baadhi kuhofu kusimama mahakamani kutoa ushahidi.
“Mtu anajua tukio zima na pengine ameona, lakini anakwambia sitaki ushahidi, siwezi kusimama mahakamani kutoa maelezo, kwa hiyo wahusika wanaachwa tu,” alisema.
“Mwananchi unakuta anawafahamu wanaohusika, lakini wanaamua kunyamaza, akiambiwa asimame kutoa ushahidi mahakamani anagoma, hii inatoa nafasi ya wanaohusika kutoa rushwa na matukio yanazimwa,” alisema.
Mtazamo wa kimila
Imani za kishirikina ndiyo sababu inayoaminiwa kuwa chanzo cha mauwaji hayo, kama inavyoelezwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania, Tonisiza Antonia.
Kwa mujibu wa Tonisiza, wapo wanaoamini mafanikio katika maisha yao yanatokana na uhai wa aina fulani ya watu, ndiyo sababu wanajihusisha na vitendo hivyo.
Mitazamo hiyo, alisema ndiyo inayosababisha matukio hayo yanatokea, yanapotea na kujirudia, akidokeza kuwepo kwa changamoto ya elimu ya utu.
Pamoja na hilo, alieleza bado hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika zinaonekana za kawaida kwa kuwa wananchi hawapati mrejesho wake, ili kutengeneza funzo kwa wengine.
“Hatua kali zinapaswa zichukuliwe kuwakomesha wanaofanya vitendo hivi. Kuwe na ufuatiliaji na ijulikane anachofanywa mkosaji isiishie kusikia amepelekwa polisi baadaye kimya,” alisema.
Sambamba na hatua hizo kali, Tonisiza alipendekeza kufanyia uchunguzi wa kina kubaini wanasiasa wanaojihusisha na imani za kishirikina kama nyenzo ya ushindi wao katika chaguzi.
Uchunguzi huo, alipendekeza ufuatiwe na kuwaweka wanasiasa watakaobainika katika kundi lililo karibu kujihusisha na vitendo hivyo, kwa sababu hawaamini katika ushindi halali.
“Mwanasiasa anayekwenda kwa mganga kutafuta ushindi maana yake hajiamini yeye na haamini ushindi wake, anatafuta nguvu ya ziada, huyu akiambiwa kafanye kitu fulani ili ushinde hataacha kufanya,” alisema.
Alisisitiza nyuma ya wanaokamatwa na kuhukumiwa kutenda makosa hayo, kunaweza kuwa na watu, akieleza umuhimu wa uchunguzi kufanywa kwa kina.
Wenye Ualbino
Mwenyekiti wa Chama Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Godson Mollel alihoji katika soko lipi viungo vya watu wenye ualbino huuzwa.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoekeza, aghalabu yanapotokea mauwaji ya watu hao, baadhi ya viungo vya miili yao hunyofolewa.
“Hivi ulimi wa mwenye ualbino unaenda kuuza wapi au unaupeleka wapi? Mkono wake unaupeleka wapi, soko la viungo vya albino ni lipi,” alihoji.
Maswali hayo, alisema ndiyo yanayotengeneza majibu kwamba kuuawa kwa watu wenye ualbino kunasababishwa na imani za kishirikina.
Kuhusu uhusiano wa kuuawa kwa watu hao na uchaguzi, Mollel alieleza ni vigumu kutenganisha kwa kuwa matukio hutokea unapokaribia uchaguzi.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, inashangaza ni zaidi ya miaka 10 sasa matukio hyo yanaendelea kufanywa, akisisitiza umuhimu wa Serikali kutafuta mbinu ya kuyamaliza.
“Sisi tumechoka, ufike wakati Serikali iseme basi imetosha, inawezekanaje yalipungua leo yanarudi tena,” alisema.
Bungeni
Kutokana na tukio la mauwaji ya Asimwe, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Khadija Taya ‘Keysha’ aliomba mwongozo kwa Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson wa kujadili namna ya kuwalinda wenye ualbino kuelea uchaguzi.
Katika msisitizo wa hoja yake hiyo, Keysha alitaka bunge liahirishe shughuli zake nyingine ili lijadili suala hilo la namna ya kuwalinda wenye ualbino kuelekea uchaguzi.
Aliijenga hoja yake hiyo akirejea tukio la Asimwe la Mei 30 mwaka huu, kadhalika alilitaja tukio lingine lililotokea Mei 4, Geita la mtoto mwenye ulemavu huo kuchomwa na kitu chenye ncha kali na watu wasiojulikana.
“Tunaitaka Serikali kuleta sheria kali zitakazoonyesha mfano kwa watu wengine kutokufanya vitendo hivi. Naomba sana kiti chako kikubali na kuridhia lakini nawaomba sana wabunge wenzangu, waunge mkono hoja hii,” alisema Khadija huku akibubujikwa na machozi.
Rais Samia aguswa
Ukiachana na mbunge huyo, masikitiko ya tukio hilo yametolewa pia na Rais Samia Suluhu Hassan mwanzo wa hotuba yake katika kongamano la sekta ya habari jana.
Aliposimama kuhutubia wahudhuriaji wa kongamano hilo, Rais Samia alisema kifo cha Asimwe kimemgusa mno.
Kwa taarifa alizonazo, alisema mtoto huyo alikuwa anacheza, akapotea na baadaye mwili wake kupatikana ukiwa umenyofolewa baadhi ya viungo.
Mkakati kuwalinda albino
Akizungumza na Mwananchi, Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime alisema jeshi hilo kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa litaendelea kutambua makundi yanayohitaji ulinzi maalum, ili kudhibiti matukio hayo kwa wenye ualbino.
Sambamba na hatua hiyo, alisema jeshi hilo litaendelea kutoa elimu kwa kushirikiana na wadau wengine, juu ya jamii kuondokana na mila potofu.
“Tutaendelea kutoa elimu kwa jamii kuondokana na kukumbatia imani potofu kwani huwezi kupata maendeleo kwa kuendekeza na kuabudu ushirikina. Siri ni ya mafanikio ni kufanya kazi halali,” alisema.
Hata hivyo, alieleza jeshi hilo litahakikisha wote waliohusika wanakamatwa, huku likiwasisitiza wananchi kutoa ushirikiano ili kufanikisha hayo.
“Kitendo cha hivi karibuni kilichotokea Mkoani Kagera cha kuchukuliwa kwa nguvu kwa mtoto mwenye ualbino na kisha kupatikana akiwa ameuawa ni kitendo cha kulaaniwa na kila Mtanzania anayethamini uhai wake na wa mwingine.
Lakini si kulaani tu bali kuungana na Serikali kuwatafuta wahusika wote waliopanga na kutekeleza uhalifu huo wa aibu na fedheha kwa nchi ambao tulishatoka huko miaka mingi,” alisema.
Kwa mujibu wa Misime, aina hiyo ya matukio hutokea kwa kuwa baadhi ya wananchi hudanganyana vijiweni kwamba kuna njia za mkato za kupata maendeleo bila kutoka jasho.
“Wanadanganyana kuwa na kiungo cha binadamu mwenzako au kubaka, kulawiti mtoto mdogo utapata mafanikio au utatajirika jambo ambalo si kweli.
“Kama kungekuwepo na ukweli katika hayo wanayodanganyana basi hao wanaoishi nao wangekuwa matajiri lakini tunachoona wanaoishi maisha ya kawaida kama tunayoishi,” alisisitiza.
Hata hivyo, alisema wote waliofanya mauwaji hayo wameishia kukamatwa, kufikishwa mahakamani na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa na wengine kufungwa vifungo vya maisha jela.
Maziko ya Asimwe
Mwili wa Asimwe aliyekutwa amefariki na baadhi ya viungo vya mwili wake kunyofolewa, umezikwa jana nyumbani kwao Muleba mkoani Kagera na kuibua huzuni kwa waliohudhuria.
Judith Richard ni mama wa Asimwe alisema kama Serikali imeshindwa kuwalinda watoto wenye ualbino inapaswa iweke wazi, huku akionyesha kusikitizwa na tukio na mwanawe.
“Serikali ijitokeze iseme ukweli kama imeshindwa kuwalinda watoto na watu wenye ualbino hapa nchini nimesikitika sana mwanangu aliporwa na leo hii nimeona mabaki ya mwili wake kweli nimezika mabaki tu,” alisema.
Akizungumza katika maziko hayo, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mjini, Erasto Sima alisema taratibu za uchunguzi zinaendelea kuwabaini waliohusika.
“Tayari Rais Samia ameagiza Serikali iendelee kufanya uchunguzi wa tukio hili na naomba kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake,” alisema. |
Haki na uwazi katika uchaguzi, maadili, afya ya akili na amani ni miongoni mwa hoja zilizopewa uzito | Haki na uwazi katika uchaguzi, maadili, afya ya akili na amani ni miongoni mwa hoja zilizopewa uzito katika hotuba za viongozi mbalimbali wa dini la Kiiislamu katika Ibada ya Eid Al-Adha na Baraza la sikukuu hiyo.
Nasaha za viongozi hao kuhusu uwazi na haki katika uchaguzi zinatokana na ukweli kwamba, imesalia miezi michache kabla ya Tanzania kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa Serikali za mitaa, utakaofuatiwa na Uchaguzi Mkuu 2025.
Jambo geni lililoibuka katika nasaha za sikukuu hiyo kwa mwaka huu tofauti na miaka mingine ni suala la afya ya akili, likitajwa na viongozi hao kama ndiyo chachu ya ukatili, matendo maovu na hata matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.
Si mara ya kwanza, katika membari za viongozi wa dini kusikia nasaha kuhusu maadili, ni jambo ambalo aghalabu huibuliwa kutokana na uhalisia wa mwenendo na tabia za watu.
Nasaha hizo zimesikika kutoka katika hotuba za viongozi mbalimbali wa dini hiyo, walipozungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ibada ya sikukuu hiyo ambayo waislamu huadhimisha tukio la Nabii Ibrahim kumtoa kafara mwanawe.
Haki katika uchaguzi
Katika nasaha hizo, iliibuka hoja ya umuhimu wa kuzingatia uwazi na haki katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu, kadhalika uchaguzi mkuu wa mwakani.
Hilo lilizungumzwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), Nuhu Mruma aliposoma risala ya baraza hilo katika baraza la sikukuu hiyo jijini Dar es Salaam.
"Tunaziomba mamlaka zinazohusika na uchaguzi kufanya kwa uwazi na weledi mkubwa huku wakizingatia utoaji wa haki kwa kila anayestahili ili tupate viongozi wanaostahili," alisema.
Sambamba na hilo, aliwasihi wagombea na vyama vya siasa kujiepusha na vitendo vya rushwa, akisema ndiyo chanzo cha kupoteza haki.
Ujumbe wa uchaguzi ulisisitizwa pia na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika baraza hilo, akisema wananchi wajitokeze kushiriki michakato yote ya uchaguzi, ikiwemo kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura.
Kadhalika, aliwataka wahakikishe wanashiriki kuchagua au kuchaguliwa, kwa kuwa ni haki yao kikatiba.
"Unayo haki ya kuchaguliwa kuwa kiongozi na unayo haki ya kuchagua kiongozi unayemtaka, hiyo ni Novemba mwaka huu," alisema.
Nasaha za uchaguzi zilisikika pia katika hotuba ya Sheikh wa Mkoa wa Pwani, Khamisi Mtupa aliyewataka waislamu kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali.
Alisema baadhi ya watendaji serikalini wanadhoofisha juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan, hivyo ni vema wenye hofu ya Mungu ajitokeze kugombea.
Ili kupatikana maendeleo, alisema ni muhimu wapatikane viongozi waadilifu.
"Changamoto iliyopo waislamu wanapenda kujiweka nyuma katika nafasi za uongozi na pale anapopewa nafasi mtu asiyefaa wanabaki kulalamika, hii haisaidii kinachotakiwa ni kujitokeza ili kutafuta nafasi na ukiipata itendee haki," alisema.
Katika nasaha zake hizo, alieleza ni vigumu kuitenganisha siasa na maisha ya binadamu, akiwashangaa wanaopinga viongozi wa dini kujihusisha na siasa.
Afya ya akili
Mjumbe wa Baraza la Ulamaa Bakwata Taifa, Sheikh Ally Ngeruko alisema matendo mengi maovu na matukio ya ukatili yanayoshuhudiwa nchini ni matokeo ya matatizo ya afya ya akili.
Alizijenga nasaha zake hizo kwa mifano ya matukio kadhaa ya wazazi kuwalawiti watoto wao, wenza kuuwana na viongozi wa dini kutenda maovu, akisema msukumo wa hayo ni kukithiri kwa matatizo ya afya ya akili.
Kwa sababu hali imefikia hivyo, Sheikh Ngeruko aliyezungumza kumwakilisha Mufti Aboubakar Zubeir alisema ni muhimu wataalamu wa saikolojia watoe elimu kuhusu afya ya akili.
"Matatizo ya akili ni makubwa, natoa wito kwa jamii, kuyatafakari haya matatizo tutaona kwamba shida kubwa ipo kwenye akili," alisema.
Maadili
Katika hotuba yake kwenye baraza la Eid Al Adha, Waziri Mkuu Majaliwa alisisitiza umuhimu wa kuimarishwa kwa taasisi ya malezi ya vijana ili kuepuka athari za mabadiliko ya sayansi na teknolojia.
Licha ya mabadiliko hayo kuja na dhamira chanya, Majaliwa alisema wapo walioyapokea vibaya na wanaathiriwa nayo, kadhalika kusababisha mmomonyoko wa maadili.
"Kila mmoja lazima aone ana wajibu wa kuwalea vijana wetu katika maadili mema," alisema.
Aliambatanisha ujumbe wake huo na kuwataka Bakwata kuzisimamia vema taasisi zinazopeleka Hija Watanzania ili wasifanyiwe ubadhirifu wa namna yoyote.
"Mimi tangu mwaka 2017 nashuhudia Bakwata ikipeleka mahujaji, mimi naomba nilisihi baraza wanaokwenda kule ni wasilamu wenzetu, simamieji weledi wa taasisi zote zinazopeleka mahujaji," alisema.
Ujumbe kuhusu maadili ulitolewa pia na Kadhi wa Mkoa wa Mbeya, Sheikh Hassan Mbarazi aliyewataka waislamu wampige vita shetani anayepotosha maadili.
Ili kufanikisha hayo, alisema ni muhimu kutumia ibada wakati wote katika kutekeleza kila jambo ikiwemo kwenye utatuzi wa changamoto.
Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Mohamed Aziz alitaka uadilifu na malezi bora kwa watoto ili kujenga maadili mema.
Alisema kwa sasa uadilifu na maadili ni changamoto kubwa katika jamii, akilaani baadhi ya viongozi wa dini kufanya vitendo visivyo vya kimaadili kwa watoto.
"Serikali inaelekeza kufanya kazi kwa maendeleo binafsi na taifa, uislamu unafundisha amani, upendo na uadilifu, lakini inasikitisha huko mikoa ya kusini wiki iliyopita sheikh mmoja ametuhumiwa kulawiti watoto 15, hii si sawa na haipendezi, kwani inabomoa uislamu wetu,” alisema.
Utunzaji Mazingira
Kauli nyingine iliyoibuliwa katika ibada ya sikukuu hiyo ni utunzaji wa mazingira, Majaliwa akiwataka Watanzania kuhakikisha wanatekeleza hilo ili kuepuka athari za mabadiliko ya tabianchi.
"Kwenye eneo hili tunajua kwamba jamii yetu wengi wetu tunapika kwa kutumia kuni na mikaa unaotokana na miti, hali hii tukiiacha na tunavyoongezeka tutakosa mvua," alisema.
Alieleza Rais Samia amekuwa mmoja wa vinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ta kupikia, ambayo ni kampeni ya dunia.
Jukumu la Watanzania, alisema ni kuhakikisha wanaungana naye kwa kutumia nishati safi ya kupikia badala ya nishati chafu.
Alisisitiza katazo kwa taasisi zinazohudumiwa watu zaidi ya 20 kuhakikisha wanatumia nishati safi kupikia.
Alieleza mwishoni mwa mwaka huu, Serikali inatarajia angalau ifikie asilimia 50 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Aliambatanisha ujumbe wake huo na kuwasihi Watanzania wajitokeze kutoa maono katika mchakato wa maandalizi ya dira ya taifa.
Alisema ni muhimu kila mwananchi mwenye utaalamu wa kila eneo ahakikishe anashiriki kutoa maoni illi yazingatiwe.
Kauli kuhusu mazingira ilitolewa na Mruma akisema miti 4,000 imepandwa na Bakwata katika Kata tano za Wilaya ya Kondoa na kwamba hilo litafanyika nchi nzima.
Matusi dhidi ya viongozi
Katika hotuba yake, Majaliwa pia aliwasihi Watanzania waache kuwasema vibaya viongozi mitandaoni, badala yake wawape moyo ili watekeleze vema majukumu yao.
"Watanzania tuache kuwafanya viongozi washindwe kutekeleza majukumu yao, badala yake tuwatie moyo wafanye kazi zao vizuri.
"Kama mnataka kutukana mtutukane sisi wadogowadogo, lakini wale wa juu kabisa waacheni watekeleze majukumu yao," alisema.
Hoja kama hiyo iliibuka katika hotuba ya Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Hassan Kabeke aliyewataka waislamu kuvikataa vyama vya siasa na wanasiasa wanaomtukana Rais Samia.
Alisema haitakuwa na maana kiongozi kukemea maadili wakati yeye ndio kinara wa kuvunja maadili, kupitia matusi anayoyatamka hadharani.
"Tunapoelekea kwenye uchaguzi nitoe wito kwa vyama vya siasa vyote kuhusu maadili, leo kuna mmonyoko mkubwa wa maadili kwa baadhi ya viongozi wa baadhi vya siasa.
“Anasimama kiongozi wa chama cha siasa anamtukana Rais, anamdhihaki Rais wa nchi masikitiko yangu baadhi ya viongozi wa dini tupo kimya hata kukemea hatukemei tunajisahau kwamba Rais ni nembo ya nchi na kwa sasa Rais ni Samia Suluhu Hassan ndiyo nembo ya nchi," alisema.
Alisema inapotokea mtu amekuwa Rais wa nchi, hapaswi kutazamwa kwa chama chake, badala yake wananchi wote wamtazame kama Amiri Jeshi Mkuu.
“Natoa wito kwa vyama vya siasa viache vinginevyo tutawashauri Waislamu na wasio waislamu wavikatae, hatuwezi kuhamasisha maadili kwa wengine wakati sisi watu wazima tunavunja maadili," alisema Sheikh Kabeke.
Hata hivyo Sheikh Kabeke alikemea kitendo cha baadhi ya watu kuchinja ng'ombe bila kuzingatia ubora wake na utaratibu wa kidini wa kumchinja mnyama huyo.
"Dhambi ni dhambi, uharifu ni uharifu hata ukijificha kwenye dini niwaombe vyombo vinavyosimamia usalama wa binadamu yako mambo yanakiukwa hata katika dini yenyewe, ng'ombe aliyechinjwa lazima awe na umri fulani, asiwe na aibu, asiwe mkondefu, Mtoto, mnyonge, asiwe amekatwa sikio lakini leo hii ng'ombe zinazochinjwa hazijakidhi viwango stahiki," alisema.
Alitaka mamlaka zinazohusika na usalama wa nyama, kuhakikisha zinasimamia uchinjaji ili kulinda afya za walaji.
"Nikiwa kama Sheikh wa Mkoa simamieni afya za wanadamu, zinanunuliwa Ng'ombe zilizo na magonjwa watu tupate maradhi sasa msiogope kukamata watu hao kwa sababu wanachinja bila hata kuwafuata viongozi wa dini.
“Watanzania tuache tamaa uwezo wa kuchinja tunao lakini naomba sheria na utaratibu ufuatwe," alisema.
Mwenyekiti wa Masjid ya Abubakar Zuber, Hamad Nchola alitoa wito kwa Mabwana na Bibi afya kuzikagua na kuchunguza Ng'ombe wanaochinjwa kwa ajili ya sikukuu hiyo ili kuepusha madhara ya kiafya kwa binadamu.
"Kuna wengine wanachinja wananyama wasio pengine unakuta ni wakondefu au wana maradhi mbalimbali hii sio sahihi kuna hatari za kiafya kwa walaji, tulidhibiti hili," alisema.
Amani
Amani ni ujumbe mwingine uliosikika katika hotuba za viongozi hao wa dini, wakitaka idumishwe kwa kuwa ndiyo msingi wa ustawi wa nchi.
Kwa mujibu wa Sheikh wa Wilaya ya Sengerema, Ahmad Ally amani na upendo ndiyo nguzo pekee ya kudumisha mshikamano miongoni mwa wananchi.
Hata hivyo, alisema kuzingatia amani ni kufuata matakwa ya dini ya kiislamu inayosisitiza suala la amani kupewa kipaumbele.
Mbunge wa Sengerema, Hamis Tabasamu ni miongoni mwa waamini wa dini ya kisiilamu walioshiriki sikuku hiyo, akiwataka waumini wa dini ya kiislamu waendelee kushikamana.
Kwa kuwa wanatarajia kujenga msikiti mpya, Tabasamu alisema ni muhimu washirikiane kulitekeleza hilo.
“Mimi ni muumini wa dini ya kiislamu, natoa Sh10 milioni kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya wa Wilaya ya Sengerema,” alisema mbunge huyo baada ya kuchangia ujenzi wa msikiti huo |
Usiri wa jamii unapofanyika ukatili kwa watoto ni moja kati ya sababu nyingi zilizotajwa na watoto w | Usiri wa jamii unapofanyika ukatili kwa watoto ni moja kati ya sababu nyingi zilizotajwa na watoto wenyewe, zinazochagiza kuendelea kwa vitendo hivyo dhidi yao.
Kwa mujibu wa watoto hao, pamoja na kundi hilo kuwa katika hatari ya kukatiliwa, aghalabu jamii imekuwa ikiwaficha wanaotenda vitendo hivyo, jambo linalowafanya waendelee.
Sambamba na mtazamo huo wa watoto, Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza umuhimu wa jamii na wazazi kuona jukumu la ulinzi wa watoto linawahusu wote.
Watoto hao walitoa kauli hizo kwa nyakati tofauti, katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika, inayoadhimishwa Juni 16, kila mwaka na kwa Tanzania iliadhimishwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kauli mbiu ya 'Elimu jumuishi kwa watoto izingatie maarifa, maadili na stadi za kazi.’
Hoja za watoto
Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Wilaya ya Kinondoni, Gift Mussa alisema usiri wa jamii dhidi ya vitendo vya ukatili kwa watoto ndio unaosababisha kundi hilo liendelee kukatiliwa.
Mussa alisema mara nyingi usiri huo hufanyika pale ambapo jamii itagundua mtoto amefanyiwa ukatili, hali aliyodai inawarudisha nyuma katika kila jambo ikiwemo masomoni.
"Tuna changamoto nyingi, lakini ya ukatili inatuathiri na inaturudisha nyuma katika maendeleo ya darasani," alisema.
Ukatili dhidi ya watoto ni miongoni mwa sababu za ongezeko la watoto wa mitaani, kama inavyoelezwa na mtoto Maria Moses anayesoma kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Mafiga, mkoani Morogoro.
Ameeleza watoto huamua kukimbilia mitaani baada ya kubakwa na wakati mwingine kulawitiwa.
Katika Mkoa wa Arusha nako, watoto wanalalamikia kuingizwa katika ndoa za utotoni na hivyo kuathirika kama ilivyosimuliwa na Felister Nicolaus (14) kupitia risala aliyoisoma katika maadhimisho hayo, mkoani humo.
Kwa mujibu wa mtoto huyo, watoto wengi nchini wameendelea kuwa waathirika wa vitendo vya ukatili kwa kutelekezwa.
“Tunaingizwa kwenye ndoa za utotoni, mambo yote haya yanaathiri malezi na makuzi yetu, kimwili na kifikra na yanakatisha ndoto zetu za maisha,” amesema Felister.
Rais Samia
Rais Samia aliadhimisha siku hiyo Ikulu ya Dar es Salaam, akiwa na watoto mbalimbali, huku akisisitiza jamii kushirikiana katika malezi bora yatakayosababisha maadili mema kwa watoto.
Alitaka hilo, liambatane na kuhakikisha usalama wa kila mtoto unakuwa jukumu la jamii kwa ujumla.
Uzalendo katika umri mdogo na elimu ni mambo mengine yaliyohimizwa na Rais Samia, alipozungumza katika maadhimisho hayo.
Akizungumzia kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga alisema urithi wa elimu ni bora zaidi kuliko urithi mali, kwa kuwa mtoto hatafilisika.
"Unapompa mtoto urithi wa elimu unakuwa umewekeza jambo kubwa kwenye maisha yake na hata akiwa mkubwa ataitumia elimu hiyo kwa manufaa yake na jamii inayomzunguka," alisema.
Kauli za Wakuu wa Wilaya
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule alisema kuna kazi ya kufanya kuhakikisha watoto wanatatuliwa changamoto zao.
"Wanakinondoni tunatakiwa kuwalinda na kuwatetea watoto katika maeneo yetu kwani Rais Samia Suluhu Hassan amebeba ajenda ya kumlinda mtoto kwa hali na mali hivyo tunapaswa kumlinda mtoto kwa kutoa taarifa,” alisema.
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Felician Mtahengewa alisema sababu kubwa ya mmonyoko wa maadili ni kukua kwa teknolojia na baadhi ya wazazi kupwaya kwenye malezi.
“Marufuku baadhi ya shule na walimu kupokea misaada ya vitabu au vitendea kazi vyovyote bila kupata idhini ya ofisi yangu , baadhi vimekuwa vikihamasisha vitendo vya mmomonyoko wa maadili,” alisema Mtahengewa.
Ofisa Ustawi wa Jamii wa kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya, Sara Ndaba alisema changamoto kwa sasa ni jinsi ya kuwaepusha watoto hasa wa mitaani dhidi ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya.
Naye, Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Alex Mkama alisema wazazi kuwaacha watoto kwenda vibanda umiza yamekuwa chanzo cha matukio ya ukatili ambapo watoto wamekuwa wakilawitiana.
“Wazazi na walezi wakiwajibika kufundisha maadili mema yatasaidia kupunguza ama kumaliza matukio ya ukatili katika mkoa huu kumuacha mtoto kujilea mwenyewe kama bata anavyolea watoto wake hiyo ni hatari,” alisema Mkama.
Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la SOS Children's Village Tanzania, Florian Fanuel alisema changamoto zinazowakabili watoto hazijabadilika shina la tatizo likaanzia kwenye malezi ya watoto ndani ya familia.
"Kuna watoto wengi wazazi wao wapo wote wawili lakini hao wazazi hawapati nafasi ya kuwalea watoto wao vizuri hivyo watoto hutoroka nyumbani,kuna familia baba au mama analea mtoto mwenyewe mazingira hayo yanatengeneza matatizo katika utoaji wa huduma bora,” alisema. |
Kuna nini Ikulu, ndilo swali linaloonekana kuwasumbua Watanzania wengi kwa sasa, baada ya Rais Samia | Kuna nini Ikulu, ndilo swali linaloonekana kuwasumbua Watanzania wengi kwa sasa, baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko mengi ya wasaidizi wake katika kipindi kifupi hasa cha Mei na Juni.
Katika kipindi cha miezi hiyo, mkuu huyo wa nchi amefanya mabadiliko ya wasaidizi wake 10, yaani wanane kwa Juni pekee na wawili amewabadilisha Mei, mwaka huu.
Mabadiliko hayo, yanahusisha kuwaondoa baadhi ya wasaidizi wake katika Ofisi ya Rais Ikulu na kuwapeleka katika mamlaka, idara na taasisi nyingine mbalimbali za Serikali.
Wakati wengi wakihoji kunani nyuma ya yote hayo, wanazuoni wa siasa na uongozi, wanahusisha mabadiliko yanayofanywa na rasharasha za kuelekea uchaguzi, kuziba ombwe la wasiowajibika na kuongeza ufanisi.
Wanataaluma wengine wamekwenda mbali zaidi na kuyafananisha mabadiliko hayo na kile walichokiita usafishaji wa nyumba iliyochafuka kitambo.
Ingawa ni mamlaka ya Rais kuanzisha na kufuta nafasi za madaraka ya namna mbalimbali katika Utumishi, kwa mujibu wa Ibara ya 36(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bado uamuzi wake unaibua mijadala.
Mijadala zaidi katika mitandao ya kijamii iliibuka katika mabadiliko aliyofanya Juni 6, 2024 alipomhamisha Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu.
Pengo katika utendaji
Katika maoni yake kuhusu mabadiliko hayo, Mchambuzi wa masuala ya siasa, Bubwerwa Kaiza alitaja mambo mawili ikiwemo changamoto ya taarifa katika ziara ya Rais Samia nchini Korea, iliyolazimu Serikali kutoa ufafanuzi.
"Nadhani kutakuwa na shida. Kwa hali ya kawaida kusingekuwa na haraka haraka kama hivi hadi wengine wanapangiwa vyeo ambavyo havina upungufu katika taasisi. Lakini nafasi zinatengenezwa ili kupata nafasi ya kuhamisha maofisa hawa,” alisema.
Maandalizi ya uchaguzi
Mchambuzi huyo kwa upande mwingine alihusisha mabadiliko yanayofanywa na Rais Samia na maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na Uchaguzi Mkuu mwakani.
"Sina ushahidi lakini nazungumza kwa uchambuzi kulingana na yanayojitokeza. Nafikiri suala la uchaguzi mwaka huu na mwaka wa kesho linaweza kuwa sababu mojawapo kwa kinachotokea, haya ni maandalizi ya watu wanaotakiwa kuwepo hapo (ofisini),"alisema Kaiza.
Mchambuzi huyo alisema kuwa katika hamisha hamiha hiyo, anadhani pengine Rais Samia anataka kuweka watendaji watakaomsaidia katika chaguzi zijazo, inawezekana watu watakaopatikana ndio watakuwasaidia katika jukumu hilo.
Anasafisha nyumba
Kwa mtazamo wa mwanahabari mkongwe, Deus Kibamba uamuzi wa Rais Samia juu ya maofisa hao waandamizi Ikulu, unasafisha nyumba iliyokuwa imechafuka.
“Nyumba imechafuka lazima isafishwe na hili halina maana ya sijui matakwa ya kiuchaguzi au matakwa ya nini. Wakati wowote katika maisha ya uongozi, nyumba inapaswa kuwa safi,” alisema.
Kwa mujibu wa Kibanda, anachokifanya mkuu huyo wa nchi ni kupanga safu ya wasaidizi wake kwa kile alichoeleza mambo hayakuwa sawa.
Hoja yake ya mambo kutokuwa sawa, inatokana na kile alichofafanua kuwa, kulikithiri usambaaji wa taarifa za upotoshaji na hakukuwa na hatua madhubuti zilizokuwa zinachukuliwa.
“Huo ni wajibu ambao baadhi ya wasaidizi wa Rais walipaswa kufanya na kuna watu pengine wameshindwa kutimiza wajibu wao huo, kwa sababu huwezi kutegemea kila wakati Rais mwenyewe ndiyo atoe majibu wakati ana wasaidizi wengi,” alisema.
Kibanda alikwenda mbali zaidi na kueleza, mabadiliko yanayoshuhudiwa yanapaswa kuwa angalizo kwa watendaji waliopo serikalini hadi sasa.
Aliwataka wajiweke sawa na kutambua wajibu wao kwani wakati wowote wanaweza kukumbwa na hatua hizo.
“Upo ushahidi wa kihistoria na kimazingira kwamba katika miaka mitatu ya Rais Samia hana hiyana katika kufanya mabadiliko, hata kwa nafasi moja katika miaka kadhaa wakabadilika watu watatu au wanne, haimpi shida” alisema.
Hata hivyo, mwanahabari huyo alisema pengine aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi ndiye anayetarajiwa kuziba baadhi ya nafasi zilizoonekana kuwa na mapengo.
“Mobhare anakwenda kupata nafasi kubwa zaidi, yenye majukumu makubwa zaidi na inawezekana ikawa ni eneo ambalo anaonekana ana nguvu zaidi na uwezo zaidi, hilo wala huhitaji kuambiwa ukisoma taarifa ya Rais inasema amepangiwa majukumu mengine,” alisema.
Alieleza hiyo inamaanisha kuondolewa kwake katika wadhifa aliokuwa nao sasa ni kwa sababu tayari kuna majukumu mahsusi aliyopangiwa.
Dk Aviti Mushi anaungana na Kibanda katika hoja kuwa, mzizi wa mabadiliko hayo licha ya kustua, lengo kuu ni kuisafisha Ikulu.
"Nadhani ameona hawawezi kuendana na kasi yake, sio viongozi wabaya lakini labda anataka kuwepo na wengine nadhani anataka kuimarisha ofisi ya Ikulu,” alidai Dk Mushi.
Dk Mushi naye aligusia suala la maandalizi ya uchaguzi kama sababu nyingine ya mabadiliko hayo akisisitiza, “Uchaguzi si lelemama.”
Wameshindwa kumsaidia
Kwa mtazamo wa Kiama Mwaimu uamuzi wa mabadiliko ya wasaidizi hao, unaweza kusababishwa na baadhi yao kushindwa kumsaidia katika anachokitarajia.
"Inawezekana pia hawa watumishi kwa mtazamo wa Rais hawawezi kumpa ushindi katika chaguzi zijazo au katika utawala bora kwenye Serikali yake," alisema Mwaimu ambaye ni mmoja wa wachambuzi wa masuala ya siasa.
Mwenendo wa pangua pangua
Pangua pangua ilianza siku chache tu baada ya Rais Samia kuapishwa kushika wadhifa huo, mwanzoni mwa mwaka 2021 akimwondoa aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Bashiru Ally na kumteua kuwa Mbunge huku nafasi yake ikichukuliwa na Balozi Hussein Kattanga Machi 31, 2021.
Aprili 4, 2021 alimuondoa Gerson Msigwa katika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, baada ya kuhudumu kwa miaka sita tangu Agosti mwaka 2016 na kumteua kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo.
Nafasi aliyokuwa nayo Msigwa ndani ya ofisi hiyo nyeti ilirithiwa na Jaffar Haniu aliyeteuliwa Juni mwaka 2021 lakini naye hakudumu, Februari ya mwaka uliofuata aliondolewa na kwenda kuwa mkuu wa wilaya Rungwe, akimpisha Zuhura Yunus.
Katika pangua pangua hiyo, Moses Kusiluka aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu na Januari 2023 Diwani Athumani aliteuliwa kumrithi. Diwani alidumu kwa siku mbili tu, baadaye nafasi hiyo ilirithiwa na Mululi Mahendeka anayeongoza hadi sasa.
Ingawa haionekani kama ni ofisi ya moja kwa moja Ikulu, lakini Agosti 28, 2023 Rais akafanya mabadiliko ya mkurugenzi mkuu wa usalama wa Taifa na kumteua Ali Idi Siwa akichukua nafasi ya Said Hussein Massoro aliyehudumu kwa miezi nane.
Tangu mabadiliko hayo, umma haukushuhudia mabadiliko ya mara kwa mara kwa wasaidizi wa Rais lakini mwezi Mei na Juni 2024 ndio miezi inaonekana kuvunja rekodi ya hamisha hamisha hadi baadhi ya watu kuanza kuhoji kuna nini Ikulu?
Hamisha hamisha siku 150
Katika mwezi Januari 2024, Rais Samia alimhamisha Afisa mwandamizi Ofisi ya Rais Ikulu, Doris Kalasa na kumteua kuwa Katibu Tawala (RAS) mkoa wa Iringa.
Mei 29,2024, Rais akamhamisha Dk Linda Ezekiel aliyekuwa Kaimu Afisa Mtendaji mkuu wa President’s Delivery Bureau (PDB) kwenda kuwa Naibu Katibu mkuu mtendaji, Tume ya Mpango nchini, anayeshughulikia ubunifu wa biashara.
Juni 6, Rais akamhamisha Felister Mdemu aliyekuwa msaidizi wa Rais (Maendeleo ya Jamii) kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii na Zuhura Yuhus kutoka mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu kwenda kuwa Naibu Katibu mkuu.
Pia tarehe hiyo hiyo, akamuondoa Petro Magoti aliyekuwa msaidizi wa Rais (siasa) kwenda kuwa mkuu wa wilaya Kisarawe na akamhamisha pia Nehemia Mandia aliyekuwa Msaidizi wa Rais (sheria) na kumteua kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.
Halikadhalika, Juni 11,2024 akamuondoa Elias Mwandobo kuwa mkuu wa wilaya ya Momba.
Juni 15,2024, akamhamisha Balozi John Simbachawene aliyekuwa Ofisa Mwandamizi Ofisi ya Rais Ikulu kuwa Naibu Katibu mkuu wizara ya Viwanda na Biashara na pia Dk Habib Kambanga mwenye wadhifa kama huo kuwa Balozi.
Pia akamhamisha Ofisa Mwandamizi wa Ofisi ya Rais Ikulu, Mkoba Mabula, kwenda kuwa Naibu Katibu mkuu katika wizara ya Maliasili na Utalii, wizara ambayo huwa nayo mawaziri wake hawadumu muda mrefu. |
Hatua ya Serikali kupendekeza msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye mafuta ya kupikia | Hatua ya Serikali kupendekeza msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye mafuta ya kupikia yanayozalishwa nchini, imetajwa kuongeza hamasa ya uwekezaji kwenye mafuta, kilimo cha mazao ya mafuta, kadhalika itapunguza bei ya bidhaa hiyo.
Wasindikaji wa ndani wa mafuta wamekwenda mbali zaidi na kueleza kwa uhalisia wa uwezo wa viwanda walivyonavyo, wanaweza kukidhi mathitaji ya ndani na hata kuuza nje mafuta ya alizeti.
Kwa mujibu wa Chama cha Wasindikaji wa Zao la Alizeti Tanzania (Tasupa), kwa sasa kuna viwanda 773 vya usindikaji alizeti vyenye uwezo wa kuzalisha tani milioni 1.7 za mafuta hayo.
Uwezo huo wa viwanda hivyo vilivyotajwa na Tasupa vinazidi mahitaji ya nchi, ambayo mwaka 2021 yalikuwa tani 650,000, huku uwezo wa uzalishaji wa ndani ulikuwa tani 290,000.
Pendekezo la msamaha wa VAT katika bidhaa hiyo inayozalishwa nchini, limetolewa juzi na Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba alipokuwa akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2024/25.
Katika wasilisho la bajeti hiyo bungeni jijini Dodoma, Dk Nchemba alipendekeza msamaha wa VAT kwenye mafuta ya kula yanayozalishwa ndani ya nchi kwa kutumia mbegu zinazozalishwa nchini kwa muda wa mwaka mmoja.
“Lengo la hatua hii ni kuendeleza unafuu wa bei ya mafuta ya kula iliyopanda kutokana na mdororo wa uchumi pamoja na vita ya Urusi na Ukraine vilivyosababisha uhaba wa mafuta hayo,” alisema.
Tanzania imewahi kupitia vipindi mbalimbali vya kupanda kwa gharama za mafuta ya kupikia na zaidi ilishuhudiwa mwaka 2022.
Katika kipindi hicho, bei ya dumu la lita 20 la mafuta hayo lilifika Sh120,000 hadi Sh130,000 kutoka Sh55,000, huku lita moja iliuzwa kutoka Sh8,000 hadi Sh9,000 kutoka Sh5,500.
Sababu ya hali hiyo, Serikali ilisema ni vita vilivyokuwa vinaendelea kati ya Urusi na Ukrain vilivyosababisha changamoto katika mnyororo wa ugavi wa bidhaa kimataifa.
Wakati wazalishaji wa ndani wakipata msamaha huo, kwa upande wa wanaoingiza kutoka nje ni maumivu, baada ya Serikali kupendekeza asilimia 35 au Dola 500 za Marekani kama ushuru wa forodha kwa kila tani moja ya bidhaa hiyo.
Pendekezo hilo ni tofauti na utaratibu uliopo ambapo, waagizaji hao hutozwa ushuru wa forodha wa asilimia 35 kwa kuagiza bidhaa hiyo mwaka mzima.
Wazalishaji wa ndani
Akizungumza na Mwananchi jana, Mwenyekiti wa Tasupa, Ringo Iringo alisema kwa sasa wasindikaji wa ndani wa bidhaa za mafuta wanatozwa asilimia 18 ya VAT.
Kodi hiyo, alisema inatozwa pia kwa wanaosafisha mafuta hayo baada ya kuyanunua kutoka kwa wasindikaji yakiwa ghafi.
Msamaha huo kwa mujibu wa Iringo, utapunguza bei ya mafuta yanayozalishwa nchini, kwa kuwa gharama za uzalishaji viwandani zitapungua.
Sambamba na kupungua kwa bei, hatua hiyo Mwenyekiti huyo alieleza itaongeza uwekezaji katika viwanda vilivyopo na kuanzishwa vipya.
“Awali, tulikuwa tunaogopa kuongeza uwekezaji kwenye viwanda vyetu kwa sababu kikiwa kikubwa tu, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inakufuata na kukutoza VAT ya asilimia 18,” alisema.
Katika mazingira hayo, alisema wawekezaji wengi walihakikisha viwanda vyao vinabaki kuwa vidogo ilimradi visikidhi vigezo vya kutozwa asilimia 18 ya VAT.
“Lilikuwa jambo la ajabu, watu wanawekeza ili kuongeza thamani mazao ya wakulima wako wewe unawawekea vikwazo vya kikodi,” alisisitiza.
Iringo pia, alizungumzia pendekezo la kutozwa ushuru wa forodha wa asilimia 35 kwa kila tani kwa mafuta yanayotoka nje, akisema utafungua soko kwa wazalishaji wa ndani.
Kabla ya uamuzi huo, alieleza waagizaji wa mafuta yaliyochakatwa kwa kiwango cha mwisho kutoka nje, waliuza kwa bei ndogo zaidi na hivyo kufanya wale wa ndani wakose soko.
“Gharama za kuagiza zilikuwa nafuu kuliko kuzalisha ndani. Tulikuwa tunahamasisha kuagiza mafuta kuliko kutengeneza mazingira ya kujitosheleza, hiki kilichopendekezwa sasa ni kitu sahihi,” alieleza.
Hata hivyo, mwenyekiti huyo alisema kilichopendekezwa na Serikali ni maoni ambayo aghalabu wamekuwa wakiyatoa kwa Serikali.
Watakidhi mahitaji
Alipoulizwa iwapo wana uwezo wa kuzalisha kiasi cha kumudu mahitaji, Iringo alieleza uwezo wa viwanda hivyo ni zaidi ya mahitaji ya nchi.
Iwapo wataachiwa, alisema wana uwezo wa kuzalisha hadi kuuza nje.
“Wakulima wengi wanashindwa kuuza mazao yao kwa sababu ya kukosa soko, soko linakosekana kwa sababu sisi tulikuwa tunabanwa, tukiachiwa tunalimudu na ziada,” alisema.
Mtazamo wa Iringo unashabihiana na Mkurugenzi wa kampuni ya G & B Soap inayozalisha mafuta nchini, Godliving Makundi aliyesema uzalishaji utaongezeka.
Kuongezeka kwa uzalishaji huko kutatokana na kile alichoeleza, gharama za uzalishaji zitapungua na hivyo wawekezaji wataelekeza fedha katika kuongeza uzalishaji.
“Uwekezaji utaongezeka kwa kuwa wazalishaji watatumia fedha ambazo wangepaswa kulipa kodi hiyo katika kuongeza nguvu za kuzalisha,” alisema.
Kwa mujibu wa Makundi, hatua hiyo pia itapunguza bei ya bidhaa hiyo kwa kuwa aghalabu wazalishaji huuza kuendana na gharama walizotumia kuzalisha.
Sambamba na hilo, mkurugenzi huyo alisema hata wakulima watahamasika kuongeza uzalishaji wa mazao ambayo ndiyo malighafi ya mafuta hayo. |
Baada ya kilio cha muda mrefu kuhusu kikokotoo hatimaye, Serikali imeongeza fao la mkupuo watakaloli | Baada ya kilio cha muda mrefu kuhusu kikokotoo hatimaye, Serikali imeongeza fao la mkupuo watakalolipwa wastaafu kutoka asilimia 33 iliyopo sasa hadi asilimia 40.
Ongezeko la fao hilo la mkupuo linajibu vilio vya wastaafu, ambao awali walilalamikia asilimia 33 waliokuwa wanalipwa, isingewasaidia kuzikabili gharama za maisha wakati wa ustaafu.
Kilio cha wastaafu kilibebwa pia na wadau mbalimbali wakiwemo wanasiasa waliodai hatua ya Serikali kuwalipa wastaafu kiasi hicho cha fao ni kukosa shukurani kwa waliolitumikia taifa kwa miaka lukuki.
Sambamba na wadau hao, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), lililalamikia hilo na kupendekeza mabadiliko ya kanuni zinazokokotoa mafao ya wastaafu.
“Kwa kuwa mifuko inaonyesha kuimarika Serikali ione haja ya kuboresha kanuni hizo bila kuathiri mifuko hiyo,” alisema Katibu Mkuu wa Tucta, Henry Mkunda alipohutubia katika sherehe za siku ya wafanyakazi duniani Mei 1, mwaka huu.
Mabadiliko ya ukokotoaji wa mafao hayo ya wastaafu, yalitangazwa bungeni jijini Dodoma jana na Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba alipokuwa akisoma hotuba ya bajeti kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2024/25.
Katika mabadiliko hayo, Dk Nchemba alisema Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza kuongezwa malipo ya mkupuo kutoka asilimia 33 iliyopo sasa hadi asilimia 40.
“Hili ndio kundi kubwa la watumishi wanaofanya kazi nzuri sana kwa taifa letu wakiwepo, Walimu, kada ya afya, Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na makundi mengine yalioko Serikali kuu na Serikali za Mitaa,” alisema.
Sambamba na maelekezo hayo, waziri huyo alieleza mkuu huyo wa nchi pia ameelekeza kuongezewa kwa fao hilo kwa kundi lililokuwa likipokea asilimia 25 na sasa litakuwa asilimia 35 kuanzia mwaka wa fedha huu.
“Mabadiliko ya kikokotoo yalishusha kundi la wafanyakazi waliokuwa wakipokea mkupuo wa asilimia 50 mpaka asilimia 33 na kundi waliokuwa wakipokea asilimia 25 walipandishwa mpaka asilimia 33,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk Nchemba, watumishi takriban 17 walioathirika na mabadiliko hayo watazingatiwa katika mabadiliko hayo.
Alisisitiza Serikali itaendelea kuangalia maslahi ya wastaafu kwa kuzingatia tathmini ya uhai na uendelevu wa mifuko.
Katika hotuba yake hiyo, alimpamba Rais Samia akisema kilichofanywa chini ya Serikali inayoongozwa naye inawapenda sana Watanzania.
Maoni ya wadau
....
Kuhusu sukari
Katika hatua nyingine, Dk Nchemba kupitia hotuba hiyo alipendekeza mabadiliko ya Sheria ya Sukari, Namba 6 ili kuwezesha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kununua, kuratibu na kuhifadhi pengo la sukari kwenye hifadhi ya chakula ya Taifa.
“Lengo la hatua hii ni kuwezesha upatikanaji wa Sukari nchini na kuondoa uhodhi kwa baadhi ya wenye viwanda bila kuathiri dhamira ya Serikali ya kulinda viwanda vya ndani,” alisema.
Kadhalika, alipendekeza kufanya marekebisho kwenye kanuni ya NFRA kwa kuijumuisha sukari kuwa sehemu ya usalama wa chakula.
Sambamba na hatua hiyo, pia Dk Nchemba alipendekeza kutoza Sh50 kwa kilo ya mabaki yanayotakana na uzalishaji wa sukari, ikilenga kuongeza mapato yatakayoiwezesha Bodi ya Sukari kutekeleza majukumu yake. |
Licha ya usafiri wa bodaboda kuwa fursa kubwa ya ajira nchini, kwa upande mwingine ni chanzo cha aja | Licha ya usafiri wa bodaboda kuwa fursa kubwa ya ajira nchini, kwa upande mwingine ni chanzo cha ajali kilichopoteza uhai wa vijana wengi, kadhalika kuwaacha baadhi yao na ulemavu wa kudumu.
Siifungamanishi hoja yangu hii na mjadala wowote kuhusu hadhi ya ajira ya bodaboda, kwa kuwa si muktadha wa ninachokiandika, bali nazungumzia pande mbili za bodaboda kama fursa ya ajira na jinamizi la ajali.
Upande wa fursa ya ajira unabaki kuwa chanya kwa kuwa, makundi ya vijana wenye viwango mbalimbali vya elimu wanashuhudiwa wakijitafutia mkate wa kila siku kupitia bodaboda, hili ni jema.
Lakini maumivu yapo kwenye upande wa chanzo cha ajali zinazosababisha vifo na ulemavu kwa vijana hao hao ambao ndiyo waajiriwa au waliojiajiri katika shughuli hiyo, ambayo baadhi ya wakosoaji wameamua kuiita ‘kukimbiza upepo.’
Kwa maoni yangu, usafiri wa bodaboda pengine ndiyo muhimu zaidi kwa safari za dharura na njia za dharura kuliko usafiri mwingine wowote unaopatikana nchini.
Kuna wakati unaweza kujiuliza na usipate jawabu kwamba kwanini mitazamo ya jamii kuhusu shughuli ya bodaboda na madereva wa usafiri huo kwa ujumla, huwa hasi.
Ukiachana na kondakta wa daladala, wanaofanya shughuli za kuzibua vyoo na waokota makopo, shughuli ya bodaboda nayo ni miongoni mwa zile zinazotolewa mifano mibaya ya kazi zisizofaa kwa watu fulani.
Mimi nimewahi kusikia mwanadada akisema, ‘nitafanya yote lakini sio ku-date yaani kujihusisha kimahusiano ya mapenzi na dereva wa bodaboda’. Alidai hawana hadhi na hawatambulishiki.
Nafahamu pengine maneno haya ni siasa za wanawake mbele ya watu, lakini nyuma ya pazia hao ndiyo mabwana zao muhimu. Lakini hatua ya mwanadada huyo kulizungumza hilo mbele ya wenziwe ni ishara kwamba si furaha yake kuonekana akiwa na uhusiano wa kimapenzi na dereva wa bodaboda.
Unadhani haya yote yanamaanisha kwamba kazi ya bodaboda ni mbaya na wanaofanya hawastahili kuheshimiwa? Hapana. Mwenendo wa wengi wao ndiyo unaoibua yote hayo.
Ni dereva wa bodaboda pekee, ndiye binadamu mwenye uwezo wa kukimbiza chombo hicho cha moto kwa mwendokasi wa 110 kwa safari ya nusu kilomita.
Ni bodaboda pekee, ndiye anayeweza kulazimisha kupenya katika eneo lenye kila dalili ya kuhitimisha uhai wake.
Ni bodaboda pekee, ndiye dereva ambaye hakuwahi kukosa haraka, wengi ukiwaona wanaharakia jambo.
Ni bodaboda pekee ndiye anayevuka barabara ilhali zimewashwa taa nyekundu, bila woga wala wasiwasi.
Kama hiyo haitoshi, ni bodaboda pekee ndiye asiyependa kuvaa kofia ngumu kwa ajili ya kulinda usalama wake, lakini atavaa tu kwa ajili ya askari wa usalama barabarani.
Hayo yote, changanya na tabia za wengi wao kujifanya wamepinda, wanaozungumza lugha yoyote mbeye ya yeyote.
Huo ulikuwa muhtasari sasa nakuja kwenye hoja ya msingi, tabia za madereva wa usafiri huo ndiyo sababu ya wingi wa ajali dhidi yao.
Baadhi ya madereva hao hupeana sifa kwa kuendesha mwendo wa kasi na kushindana wakiwa barabarani, huku wengine wakiwa wanachomekea katikati ya magari bila kujali kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha yao.
Uhalisia wa jambo hili unaonekana kwenye takwimu za Jeshi la Polisi Kikosi cha usalama barabarani kuwa hadi mwaka 2019 nusu ya ajali zilizotokea nchini zilisababishwa na uzembe wa madereva.
Hii inamaana katika kila ajali 10 zinazotokea nchini tano zilisababaishwa na uzembe wa madereva. Takwimu hizo zilifafanua zaidi kwamba katika madereva watano waliosababisha ajali wawili ni madereva bodaboda.
Si hivyo tu, hata katika takwimu zilizotolewa na Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) mwaka jana zilionyesha kati ya majeruhi wa ajali waliopokelewa, wa bodaboda watu 9 hadi 10 kwa siku ambapo ni sawa na 70 kwa wiki na 280 kwa mwezi.
Na katika kuliwekea msisitizo hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dk Respicious Boniface alisema kuna ongezeko la ajali hususan za pikipiki ambazo zinasababishwa na kutofuatwa kwa sheria za barabarani ambapo wahanga wengi hawavai kofia ngumu (Helment).
Ni wazi kuwa Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha suala hili linapungua kwa kutoa mafunzo kwa madereva hao.
Mafunzo hayo, yanalenga kupunguza ajali hizo lakini bado jitihada zaidi zinahitajika kutoka kwa Serikali na taasisi binafsi ili kuokoa maisha ya vijana wengi wanaopoteza maisha.
Muhimu pia ni namna ya utoaji wa elimu hizo za usalama barabarani kwa madereva uwe rafiki kiasi kwamba kila dereva aone askari wa kikosi cha usalama wa barabarani ni rafiki yake.
Aidha kama njia hizo pia zinachukua ugumu kutekelezwa, Serikali ichukue hatua za haraka kuwanusuru vijana wanaopotea kwani wengi wao wana umri mdogo hivyo, taifa linapoteza nguvu kazi ambayo ingesaidia katika kulipeleka mbele taifa. |
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetangaza kuanza kwa safari za mwanzo za treni ya mwendokasi kutoka | Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetangaza kuanza kwa safari za mwanzo za treni ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kuanzia Juni 14, mwaka huu.
Kuanza kwa safari hizo kunafanyika karibu wiki mbili kabla ya siku ambayo Rais Samia Suluhu Hassan atazindua rasmi safari ya treni hiyo, Juni 25, mwaka huu.
Hata hivyo, safari za treni hizo zinaanza ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya ule ambao Rais Samia Desemba 31, mwaka jana aliiagiza TRC kuhakikisha treni hizo zinaanza kusafirisha abiria kuanzia Julai mwaka huu.
Kwa mujibu wa TRC, mwanzo wa safari hizo ni ishara ya kuimarika kwa miundombinu ya usafirishaji, itakayochochea ukuaji wa uchumi wa kanda.
Hayo yalielezwa jana na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa wakati wa kampeni ya uzinduzi wa huduma za uendeshaji wa SGR, iliyopewa jina la “twende tupande treni yetu, tuitunze, tuithamini”.
"Tumezindua kampeni iliyopewa jina la kuhamasisha watu wengi zaidi kusafiri kwa treni ili wakati wa operesheni rasmi za reli ya SGR Dar es Salaam -Dodoma watu wengi zaidi waifahamu na itazinduliwa Julai 25, na Rais Samia,” alisema.
Alisema TRC imeanza na Dar es Salaam- Morogoro kama hatua ya awali zitakazowezesha kupata uzoefu na kutatua changamoto zitakazojitokeza ili kuboresha safari zitakazoendelea.
Katika kauli yake hiyo, Kadogosa alisema nauli za treni ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam-Dodoma, kwa daraja la uchumi ni Sh70, 000, biashara Sh100,000 na daraja la kibiashara la kifalme ni Sh120,000.
"Kulingana na mahitaji ya soko la wateja, TRC imepanga kuanza na treni mbili kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma na Dodoma hadi Dar es Salaam kila siku," alisema.
Kuhusu usalama, alisema utakuwepo wa uhakika kwa kuwa vichwa vya treni hizo vimefungwa CCTV Kamera zitakazowezesha abiria kufuatiliwa akiwa ndani na wakati wa kushuka.
Alieleza doria hiyo itafanywa katika safari yote, ili kudhibiti wale wasio waaminifu kuhatarisha usalama kwa namna yoyote.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TRC, Jamila Mbarouk aliliambia Mwananchi kuwa njia ya Dar es Salaam - Morogoro itaanza na nauli zilizotangazwa hivi karibuni na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (Latra).
Ofisa Biashara wa TRC, Lilian Mselle alisema njia mbalimbali zitatumiwa na abiria kununua tiketi ikiwemo Gepg (control number), Visa au Master card na kupitia mitandao mbalimbali ya simu.
"Hatua hii inalenga kupunguza malipo ya fedha ya mkono kwa mkono na kuhamasisha malipo kwa njia ya mtandao. Chakula kitauzwa kwenye vituo kwa bei nafuu kwa, sababu hiyo hakuna abiria atakayeruhusiwa kuingia kwenye treni na chakula,” alisema.
Watakaoruhusiwa kuingia na vyakula ni wanawake wanaonyonyesha na vyakula hivyo vinapaswa kuwa vya watoto wenye umri wa kuanzia miezi sita hadi mwaka mmoja.
Alisema katika daraja la biashara, abiria ataruhusiwa kubeba mzigo wa kilo 20 bure.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Tanzania (TCB), Adam Miyaho alisema wameamua kushirikiana na TRC kuhakikisha wanaleta mapinduzi katika sekta ya uchukuzi.
“Tumeshirikiana na TRC kwa kukusanya nauli. Tuna matumaini kwamba kila mtu ataangalia SGR kama fursa ya kuwekeza," alisema.
Mkuu wa Mradi wa Yapi Merkezi, Mehmet Firat alisema kuanza kwa safari hizo ni historia kwani ni mradi walioanza kujenga tangu awali.
"Tumejenga SGR Dar es Salaam-Morogoro na kila kitu kimekamilika tunatarajia itatumika kukuza uchumi wa nchi," alisema.
Kwa mujibu wa Mehmet, Tanzania imejenga SRG bora zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, ikiwa ni hatua kubwa kwa wananchi wake na sekta binafsi kuitumia. |
Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu kusimama imara katika mchakato | Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu kusimama imara katika mchakato wa mageuzi wa mashirika ya umma na kupuuza kelele atakazokutana nazo kwenye mageuzi hayo.
Rais Samia amesema anafahamu mchakato huo ni lazima uhusishe kelele kwa kuwa kuna watu watakaoumizwa na mageuzi hayo lakini ni lazima yafanyike kwa mustakabali wa uchumi wa Taifa.
Alifananisha hilo na mfano wa kile alichokiita kelele zilizopigwa dhidi yake wakati wa mkataba wa ukodishaji bandari kati ya Serikali na DP World, akisema hatimaye sasa matokeo chanya yanayonekana.
Kutokana na ushirikiano huo na sekta binafsi katika uendeshaji wa bandari, Rais Samia amesema umeiwezesha Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), kutoa gawio kubwa la Sh153.9 bilioni.
Maelekezo hayo aliyatoa jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kupokea gawio na michango kutoka kwa mashirika ya umma ambapo Serikali ilipokea Sh637 bilioni kutoka kwa mashirika na taasisi 10.
Akizungumza baada ya kupokea gawio hilo Rais Samia alioneshwa kutoridhishwa na utendaji wa mashirika ambayo yanamilikiwa na Serikali na kumpa changamoto msajili wa hazina kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kunakuwa na matokeo chanya.
Alisema Tanzana haina budi kufanya mageuzi ya kiuchumi na mchakato wa kufanya mageuzi hayo ni lazima uhusishe mashirika na taasisi za umma.
“Mchechu fanya kazi yako najua utalaumiwa lakini hiyo ndiyo kazi niliyokupa simama ifanye, mimi kazi niliyopewa na Watanzania nimesimama naifanya na mnashuhudia matusi ninayotukanwa mpuuzi, hana maana, huyu bibi yani mambo tele lakini najigeuza chura.
“Kelele nyingi zinapigwa, wakiona kimya wanaona wanitukane kama nitajibu, sijibu ninachotaka ni mageuzi ya kiuchumi katika nchi hii sasa kwenye hayo mageuzi kuna watakaoumia. Anayetaka kunikera mimi anikanyagie uchumi wangu, katika mageuzi haya tutawakanyaga wengi wale ambao hawataki kwenda mbele na ndiyo hao watakaopiga kelele.”
Katika hilo alisema hatokuwa na uvumilivu kwa mashirika ya Serikali ambayo yamebweteka yakisubiri msaada kutoka serikalini na kuwataka wajifunze kutoka kwenye mashirika ambayo Serikali imeingia ubia na sekta binafsi.
“Kampuni zilizotoa gawio ni zile ambazo Serikali ina hisa chache kwa maana hisa nyingi ni za sekta binafsi, zile za Serikali hazipo hapa lakini sera ni zile zile ila kampuni zetu zimebweteka.
“Sekta binafsi wanahangaika kwa kutumia mbinu zote za biashara ili waweze kupata faida, hapa kuna somo kwa mashirika yetu. Lengo kwenye gawio ni asilimia 11 lakini tupo asilimia 3 ambayo tulikuwa nayo mwaka jana ni imani yangu kuwa mwakani tutasogea. Tutasogea endapo mashirika 159 ambayo hayakutoa gawio mwaka huu nayo yatajituma kufanya kazi yaweze kuchangia Serikali.”
Rais Samia alisema ataendelea kusimamia na kufuatia kwa ukaribu ajenda ya mabadiliko katika mashirika ya umma na kamwe hatoyumbishwa na maneno yanayolenga kumtoa kwenye reli.
Akitolea mfano wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ambayo imetoa gawio la Sh153.9 bilioni, Rais Samia alisema mafanikio hayo ni matokeo ya uwekezaji uliofanyika bandarini ambapo tayari kuna wawekezaji wawili.
“Pale TPA mwaka jana kiwango hakikuwa hiki, lakini kwa mageuzi makubwa yaliyofanyika bandarini mwakani tunatarajia makubwa zaidi. Bandarini kuna watu wawili hivyo tunatarajia makubwa, wale waliopiga kelele mama kauza bandari, mara kauza bahari mauzo yale faida yake ni hii leo na huu ni mwanzo tunatarajia kupata makubwa zaidi kwa bandari zote.” alisema Rais Samia.
Wajumbe wa bodi
Rais Samia alibariki mchakato wa upatikanaji wa wajumbe wa bodi wa mashirika kupatikana kupitia ushindani utakaohusisha elimu na uzoefu wao.
“Sasa wajumbe wa bodi watashindanishwa, yale mambo ya kutaka kuingia kwenye bodi kwa sababu umekuwa nje kwa muda mrefu yamekwisha. Mimi niachieni hawa wenyeviti nitateua kulingana na sifa na vigezo ila wajumbe washindanishwe,’;
Agusia hofu ya mageuzi
Alisema miongoni mwa mambo yanayokwamisha jitihada za kuyainua mashirika ya umma ni hofu inayotengenezwa na baadhi ya watendaji wanaohisi mageuzi hayo yakitokea yataziba mirija yao.
“Tunachotaka ni matokeo chanya hatuna sababu ya kuhofia mageuzi yanayoendelea, hii inanikumbusha ndani ya chama changu nilivyotoa wazo la vyama vya siasa viachwe vifanye siasa nilishambuliwa kwenye kamati kuu wakihofia itakuwaje lakini tulipowafungulia wamefanya nini. Hatuna sababu ya kuwa na hofu”.
Taarifa ya gawio
Akitoa taarifa ya gawio, Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu Sh637 bilioni zimepokelewa ikijumuisha gawio la Sh279 bilioni kutoka mashirika ya biashara na michango ya Sh358 kutoka katika taasisi nyingine.
“Makusanyo haya ni ya kipindi cha kuanzia Julai 2023 hadi Mei 2024, hata hivyo kwa kuwa mwaka wa fedha 2023/24 haujakamilika, makusanyo bado yanaendelea na tunatarajia kufikisha Sh850 bilioni,” alisema.
Aliyataka mashirika yanayodaiwa kuhakikisha yanakamilisha malipo ya gawio hilo kabla mwaka wa fedha haujaisha.
Hata hivyo, alisema jumla ya waliotoa gawio hilo ni 145, ikiwa ni ongezeko la mashirika 36 kutoka 109 yaliyochangia mwaka jana.
Alisema mashirika 159 hayajachangia katika mfuko mkuu wa Serikali kwa mwaka huu, akiyataka kubadilika na kuboresha utendaji wao wa kazi utakaowezesha kuchangia.
“Kuchangia katika mfuko mkuu wa serikali sio suala la fadhila ni suala la lazima na wajibu wa kisheria,” alisema.
Katika gawio la mwaka huu, alisema kunaibuka swali la kwanini taasisi za kibiashara za Serikali hazipo katika 10 bora ya uchangiaji wa faida.
Kuhusu mchanganuo wa gawio hilo, taarifa ya Mchechu iliweka wazi kuwa, kampuni za biashara ambazo Serikali inamikiki hisa chache ikiongozwa na NMB Bank PLC ambayo Serikali inamiliki asilimia 31 na imechangia Sh54.5 bilioni.
Nyingine ni Twiga Minerals Corporation ambyo Serikali inamiliki asilimia 15 ya hisa na imechangia Sh53.4 bilioni, huku Airtel Tanzania ambayo Serikali inamiliki asilimia 49 ya hisa na imechangia Sh40.8 bilioni.
Kampuni ya Puma Energy, Serikali inamiliki asilimia 50 ya hisa na imetoa gawio la Sh12.2 bilioni, huku TPC inayomilikiwa na Serikali kwa asilimia 25 na imechangia Sh10.2 bilioni.
Kwa upande wa taasisi zinazochagia asilimia 15 ya mapato ghafi na michango mingineyo serikalini, taarifa hiyo imeeleza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) imetoa gawio la Sh153.9 bilioni
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Tanzania (TCRA), imetoa gawio la Sh34.7 bilioni, huku Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), ikitoa Sh21.3 bilioni.
Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), imetoa gawio la Sh19.1 bilioni, huku Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), ikitoa gawio la Sh18.9 bilioni. |
Kama umewahi kuwasikia waswahili wakisema kisicho riziki hakiliki, basi methali hiyo imeakisi uhalis | Kama umewahi kuwasikia waswahili wakisema kisicho riziki hakiliki, basi methali hiyo imeakisi uhalisia katika familia ya Kwangaya yenye makazi yake Rufiji mkoani Pwani.
Familia hiyo iliyokuwa katika matarajio ya mipango ya harusi, ghafla mpango huo umegeuka huzuni, baada ya aliyetarajiwa kuolewa kupoteza maisha.
Bi harusi huyo mtarajiwa ni mmoja kati ya ndugu wanne wa familia moja walipoteza maisha katika mafuriko yaliyotokea Rufiji mkoani Pwani.
Mafuriko hayo yaliikumba Wilaya hiyo ya Rufiji kuanzia mwanzoni mwa Mei mwaka huu na kufuatiwa na Kimbunga Hidaya.
Mzizi wa mafuriko hayo ni mfululizo wa mvua kubwa zilizonyesha katika maeneo mbalimbali nchini kwa takriban miezi saba, kama zilivyotabiriwa na Mamalaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
Ilivyotokea
Akisimulia mkasa ulioondoa uhai wa bi harusi huyo mtarajiwa na wengine watatu, Jamal Kwangaya ambaye ni baba yake mdogo anasema maisha ya mwanawe huyo yalikuwa katika Kijiji cha Mope, eneo ambalo lilikuwa maalum kwa shughuli za kilimo.
Ingawa Kijiji hicho ni hatari kwa maisha ya binadamu hasa nyakati za mvua kubwa, anasema walilazimika kuendelea kubaki huko kwa kuwa ilikuwa vigumu kupata mtumbwi wa kuwahamisha.
Baadaye anaeleza mafuriko yalikiathiri Kijiji hicho na hivyo, walilazimika kuhamia ng'ambo yake katika Kijiji cha Kongoniongo.
"Kipindi cha maafa mtumbwi ilikuwa vigumu kupatikana, wale wakakwama kule katika maeneo yaliyopaswa kuhama," anasema.
Waliishi katika eneo hilo hadi ulipofika wakati mahitaji muhimu ya binadamu yalipokwisha na kwa kuwa walitumiwa fedha walitakiwa kwenda kuitoa ili kununua mahitaji hayo.
Hawakuwa na namna nyingine zaidi ya kutafuta mtumbwi wa kuwawezesha kufika Ikwiriri, kwa kuwa katika Kijiji hicho hakukuwa na huduma za kifedha.
"Mahitaji yalishaisha sasa wakawa wanalazimika wake huku (Ikwiriri) kwa sababu kuna salio walitumiwa kwa simu walilazimika wake huku wapate mahitaji, alafu wazunguke njia ya Utete hadi Utunge ndiyo wapige simu wafuate kurudi kijijini," anasema.
Anaeleza katika harakati za kwenda Ikwiriri walifanikiwa kupata mtumbwi na walipanda watu nane wakiwemo sita wa familia moja.
"Walipanda hadi walipofika darajani mmojawao wa kiume alitaka kushushwa darajani na dereva wa mtumbwi aliwataka wote washuke darajani hapo.
"Lakini wakakataa kwa kuwa hawakuwa na fedha ya kutokea eneo hilo hadi Ikwiriri hivyo waliomba kuendelea na safari na mtumbwi hadi eneo la jirani na Ikwiriri," anasema.
Safari na mtumbwi wenye abiria saba iliendelea hadi walipolifikia daraja la Rufiji kwanza na hapo ndipo mzizi wa ajali ulipoanza.
"Yule dereva hakuwa anajua kama pale kwenye daraja kuna asilimia ya maji ya mzunguko kwa hiyo yakawa yanamvuta, alionekana umemshinda.
"Akawa anashauriwa kupita chini ya daraja naye anatekeleza hilo na alivyopika mbele mzunguko wa maji ulizidi hadi kusababisha mtumbwi kupinduka," anasema.
Baada ya mtumbwi kupinduka, anasema waliozama ni mwanawe na wajukuu zake wanne, lakini mmoja aliokolewa.
Baada ya hatua hiyo, hatua za kutafuta miili ya waliozama ziliendelea kwa siku tatu bila mafanikio.
Anasema siku ya nne kwa kushirikiana na Serikali ndipo walifanikiwa kupata miili miwili ya ndugu zao wakiwa wamefariki.
Kesho yake tena, anaeleza ulionekana mwili wa ndugu yao mwingine, na mwili mmoja haukupatikana hadi sasa.
"Hiyo maiti ya mdogo hatukubahatika kuiona hadi hivi sasa, kwa hiyo tunashukuru kwa Serikali kutusaidia na kushirikiana na wananchi katika yote," anasema.
Anasema aliyefariki pamoja na ameacha familia kwa maana mtoto mmoja, baba na dada yake ambao yeye ndiye aliyekuwa mlezi wao.
Nje ya ndugu hao, anasema wamepoteza mazao mbalimbali ikiwemo ufuta katika mashamba ambayo yote yamesombwa na mafuriko.
Kuhusu harusi
Kwa mujibu wa Kwangaya, hadi mwanawe huyo anafariki dunia hakuwa na mume, isipokuwa kulikuwa na taarifa ya matarajio ya ndoa.
Anasema kabla ya kufariki mwanawe huyo alishamtaarifu kwamba siku chache zijazo angempa taarifa rasmi juu ya kupatikana kwa mchumba lakini hilo halitakuwepo tena.
"Kipindi ambacho alikuwa anakuja huku kulikuwa na taarifa ya ndoa na kwa sababu wakati wake umefika ndoa imeishia hapo. Kwa hiyo hilo tulilijua kwamba kulikuwa na mchumba anayehitaji kumuona," anasema Kwangaya.
Maisha baada ya msiba
Anaeleza maisha ya familia nzima wameendelea kuwa magumu hasa baada ya msiba wa ndugu hao kwani mazao yote waliyotarajia kwa ajili ya chakula yamepotea.
Hali inakuwa mbaya zaidi kwa kile alichoeleza, hata mahindi waliyoyapanda baada ya mafuriko hayo, nayo yamesombwa tena na maji.
"Watu siku mbili tatu hizi tukajaribu tena kwenda kupanda mahindi, leo kwa taarifa niliyonayo ni kwamba kuna maji yameyapitia nusu. Tunaiomba sana Serikali jicho lake liangalie Rufiji hasa Ikwiriri," anasema.
Shangazi wa marehemu
Mtumwa Mbonde ni shangazi wa marehemu anasema alipokea taarifa ya msiba kwa simu aliambiwa ndugu zake hao wamezama maji.
Baada ya taarifa hiyo, anasema walitafutwa askari wa zimamoto kwa ajili ya uokoaji hawakufanikiwa hadi siku tano baadaye ndipo walipofanikiwa kuiona miili ya wawili na baadaye mmoja na mwingine hadi sasa haujapatikana.
Anaeleza huyo mkubwa aliyefariki alikuwa mkulima na kwamba kifo chake kimeacha majonzi kwani ni vigumu kusahau.
"Ni msiba mzito hatutausahau kwa sababu ni pigo kubwa," anasema.
DC Rufiji
Akizungumzia vifo kutokana na mafuriko, Mkuu wa Wilaya hiyo, Meja Edward Gowele anasema jumla ya watu tisa wamepoteza maisha katika Wilaya hiyo.
Anaeleza awali kabla ya Kimbunga Hidaya walifariki wawili akiwemo mwanamke mwenye umri wa miaka 20 na mtoto wa miezi miwili.
Vifo hivyo, anasema vilifuatiwa na vingine vya wanne na ndivyo hivyo vya familia moja.
"Kwa ujumla tulikuwa na vifo tisa vilivyotokana na wananchi kutumia mitumbwi ilhali Serikali ilishakataza. Lakini kwa maji kuzingira nyumba hakuna mtu aliyepoteza maisha," anasema.
Hata hivyo, anasema iwapo wananchi wagezingatia miongozo waliyopewa na Serikali ya kuacha kutumia mitumbwi pengine wangeokolewa.
Historia ya mafuriko Rufiji
Ingawa yaliyoshuhudiwa mwaka huu yalikuwa na athari kubwa zaidi, lakini historia inaonyesha hii si mara ya kwanza kwa Wilaya hiyo kukumbwa na mafuriko.
Inaelezwa Wilaya hiyo imekuwa katika hatari ya kuathiriwa na mafuriko katika nyakati tofauti kama inavyoelezwa na Faraji Maloa Mkazi wa Rufiji kwa miaka 40 sasa.
"Nafahamu habari hizi za mafuriko mara ya kwanza mwaka 1936 kulikuwa na mafuriko makali yaliitwa Lilale na ndiyo yaliyotengeneza mito mbalimbali.
"Kwa mfano Daraja Ngayonga, Mtanga, Tingetingeni, Ruwoyi yote hayo ni zao la mafuriko hayo," anasema.
Anaeleza mafuriko hayo ya mwaka 1936 ndiyo yaliyotengeneza Ziwa la Umwe na mito Lingola, Urungu, Poka na Kingola.
Mito na mifereji hiyo yote kwa mujibu wa Maloa, imekuwa vyanzo vya mafuriko mvua kubwa inaponyesha.
Pamoja na eneo hilo kuwa hatari kwa mafuriko, anasema watu wanalazimika kuishi kwa kile alichoeleza, wanafuata rasilimali ardhi yenye rutuba.
"Unajua bonde ni ardhi yenye rutuba sana kwa hiyo mtu hawezi kuiepuka hiyo lazima atakwenda kwenye ardhi yenye rutuba huwezi kwenda kulima kwenye ukame," anasema.
Alivyoathirika
Tangu mvua zilivyoanza Oktoba mwaka jana, anasema hakuna aliyetilia maanani hadi pale Serikali ilipotoa taarifa ya tahadhari.
Anaeleza kuanzia Aprili, tahadhari hiyo ya Serikali ikawa katika uhalisia, wananchi walianza kushuhudia mafuriko katika mashamba na makazi yao.
"Mimi nilikuwa na ekari 12 zote zilijaa mpunga zote zimesombwa na mimi ndiyo nilikuwa nategemea hizo tu kwamba nikivuna nitakuwa na fedha na chakula cha kutosha," anasema.
Anaeleza hata kama wanahitaji msaada, lakini ni vigumu kuupata utakaowatosheleza kwa kuwa idadi ya wanaoishi eneo hilo ni wengi.
Mbali na Maloa, Mkuu wa Wilaya hiyo, Meja Gowele anasema watu 89,000 wameathirika wanaojumuisha kaya 23,360.
Anaeleza nyumba 628 zimeathirika katika Kata 12 kati ya 13 zinazopatikana wilayani humo, akisisitiza hiyo ni kabla ya Kimbunga Hidaya.
Apendekeza suluhisho
Kwa sababu ni vigumu wananchi kuhama kutoka katika maeneo hayo yenye ardhi nzuri, Maloa anasema ni muhimu wangekuwa wanapewa taarifa mapema kuhusu misimu ya mwaka.
"Mafuriko yameanza tangu Aprili, Serikali ilikuwa haioni kama kuna mafuriko? Kuwataarifu watu wawe tayari kwamba mwezi kadhaa na mwezi kadhaa tuwe tayari kupokea mafuriko," anasema.
Anasema ni vigumu kuhama eneo hilo kwa kuwa ndiko wanakopatia riziki zao.
"Tumeambiwa tuondoke kule katika bondeni ambalo limefunikwa kabisa na maji, lakini yatakuja kwa sababu gani ni kwa sababu bwawa la Mwalimu Nyerere limejaa kupita kiasi," anasema.
Anasisitiza umuhimu wa taarifa kutolewa mapema ili wananchi wajipange mapema na hilo lisifanywe na Mkuu wa Wilaya pekee, bali kila ngazi.
Akizungumzia hatua za muda mrefu kudhibiti athari, Mkuu wa Wilaya hiyo, Meja Gowele anasema Serikali iliomba eneo la ekari 150 katika msitu wa hifadhi kwa ajili ya kuanzisha makazi.
Anaeleza tayari baadhi ya wananchi wameanza kuingia katika eneo hilo na wengine wanaendelea, ili kuepuka athari za mafuriko kwa siku zijazo.
Kwa mujibu wa Meja Gowele, katika Kijiji cha Tungi viwanja vinaendelea kutolewa kwa wananchi ili wakaishi katika maeneo hayo ambayo kimsingi ni salama.
"Tunataka wahamie kwenye hayo maeneo ilk watoke mabondeni waje waishi mahala salama. Kuna maeneo tumetoa bure na kuna ambayo wanachama gharama kidogo," anasema.
Anasema hamasa imetolewa kuhakikisha wananchi hawarudi katika maeneo yao ya awali, ambayo ni hatari kwa mafuriko.
Kuhusu misaada, anasema watu 498 walikosa makazi hivyo Serikali ilipeleka mahema 12, chakula zaidi ya tani 200 kwa ajili ya kuhudumia watu waliopo kwenye kambi na wale waliopo kwa ndugu jamaa na marafiki.
Pamoja na Serikali, anasema misaada mwingine ililetwa na Mbunge wa Rufiji, Mohamed Mchengerwa na hivyo kutosheleza wakazi wa eneo hilo.
"Hivi juzi ameleta misaada ya mbegu zenye thamani ya Sh40 milioni kutoka kwenye mfuko wake mwenyewe na ametafuta wahisani CRDB wametuletea mbegu za Sh40 milioni," anasema.
Anaeleza bado usambazaji unaendelea kuhakikisha zinatosheleza mahitaji. |
Safari ya mwanafunzi Khadija Makalani kuhitimu elimu ya msingi huenda ikaishia njiani, baada ya kuko | Safari ya mwanafunzi Khadija Makalani kuhitimu elimu ya msingi huenda ikaishia njiani, baada ya kukosa Sh10,000 ya kununua sare za shule.
Mwanafunzi huyo wa darasa la sita katika shule ya Msingi Myumbu wilayani Kilwa katika Mkoa wa Lindi, amejikuta katika hali hiyo baada ya sare za shule alizokuwa nazo kusombwa na maji.
Hayo yote ni sehemu ya maisha ya Khadija na familia yake baada ya athari za mafuriko yaliyokikumba Kijiji cha Myumbu Mei 4, mwaka huu.
Khadija ambaye ni mmoja kati ya wajukuu sita wa bibi yake, Mariam Gumba amekatisha masomo kwa takriban wiki nne sasa tangu sare hizo ziliposombwa na maji.
Sare ilivyopotea
Katika simulizi yake kuhusu mkasa wa kusombwa kwa sare yake ya shule, Khadija anasema ilikuwa mchana wa Mei 4, mwaka huu.
Siku hiyo kwa mujibu wa Khadija, nyumbani walikokuwa wanaishi kuliingia maji kutokana na mafuriko yaliyokikumba kijiji hicho.
Mafuriko hayo, pamoja na vitu vingine vilivyokuwepo ndani, yalisomba pia sketi yake ya shule ambayo ndiyo iliyokuwa sare tegemezi kwake.
"Mvua ilianza Ijumaa hadi jumamosi yakaja mafuriko. Sikwenda shule nilikuwa naogopa kuvuka maji yalikuwa mengi. Nikawa sijaenda shule, nguo yangu ikaondoka na maji," anasema.
Lakini baada ya mkasa huo, Khadija anasema alimpata msamaria mwema aliyempatia sketi kwa ajili ya kuendelea na masomo.
Hata hivyo, sketi hiyo haikuwa mpya, hivyo ilichukua siku chache kuchanika kiasi cha kushindwa kushoneka.
"Nikaletewa nyingine (sare) nikaendea shule, nilipewa tu huko Somanga, lakini ya zamani alinigea dada Amina," anasema.
Anaeleza kuondoka kwa sketi yake ya shule ulikuwa mkasa wa pili baada ya kuondokewa na shati lake siku kadhaa kabla ya mafuriko.
Kwa mujibu wa Khadija, shati hilo liliondoka alipokuwa akivuka mto kurudi nyumbani na kwa sababu ulijaa maji.
Katika harakati za kujiokoa asisombwe na maji mtoni hapo, binti huyo mwenye umri wa miaka 12 akashindwa kulitetea shati lake.
"Nilivaa nguo za kuvukia za nyumbani, ndiyo shati likaondoka na maji nikirudi tena nyumbani sijaenda," anasema.
Hali imekuwa mbaya zaidi, baada ya kukosa fedha kiasi cha Sh10,000 kwa ajili ya kununua sare hizo na bibi yake anaeleza magumu wanayopitia baada ya mafuriko.
Bibi yake asimulia mkasa
Mariam ambaye ni Bibi wa Khadija anasema katika nyumba yao, wanaishi watu saba na mafuriko yalipotokea yaliondosha sehemu kubwa ya mali zao.
Anaeleza ni vyombo vichache tu ndivyo walivyofanikiwa kuviokoa, lakini si kuku wala mali nyingine.
"Tulilala nje ya nyumba yetu kwa siku tano na baadaye tuliomba hifadhi kwingineko na tumepewa muda hadi Oktoba 5, mwaka huu tuwe tumeondoka," anasema.
Hata hivyo, Bibi huyo anasema hadi sasa hafahamu wapi watakwenda na familia yake baada ya kumaliza siku walizopewa kuishi katika makazi hayo ya muda.
"Hadi leo hatujaelewa tutaenda kukaa wapi, kwa kuwa kuanza kujijenga hadi kupata nyumba, hali ngumu ndiyo tupo hapa tunashangaa tufanye nini," anasema.
Mariam anasema maisha yake na familia hiyo yamekuwa kizungumkuti kwani hana mtu wa kwenda kufanya kazi kusaka mlo zaidi yake.
"Nimezaa watoto tisa sio kwa mume huyu, Baba yao amefariki watoto ninao, lakini hao wakubwa Mungu hakunijaalia wawe na akili ya kunisaidia," anasema.
Shughuli za kilimo ndilo tegemeo pekee la Mariam kwa ajili ya kulea familia hiyo na hata hivyo mazao yote yamesombwa na maji.
"Kilimo chenyewe ndiyo hivyo maji yameondosha ndiyo hivyo matatizo yameingia. Shambani tulilima mipunga, mihogo na yote imeharibika kwa sababu ya mafuriko," anasema.
Hali hiyo kwa mujibu wa Mariam, imebadili ratiba ya mlo wa familia yake kutoka mara mbili kwa siku hadi mara moja kwa baadhi ya siku.
"Kwa kuwa maisha yenyewe yashakuwa magumu, unaweza ukakaa hadi saa nane mchana ukapika ugali mkala, jioni ikipatikana sawa ikikosekana hamna shida," anasema.
Jirani alivyowapokea
Hassan Kingoma ni jirani aliyewahifadhi Mariam na wajukuu zake katika nyumba yake, anasema siku hiyo ilikuwa hekaheka.
Kwa sababu katika eneo lake ni vigumu maji kufika, anasema aliamua kuwasaidia majirani kutoka katika maeneo yao na kwenda hapo.
Wakati wanaokoa baadhi ya vyombo kwa Mariam, anasema ulifika wakati maji yalijaa usawa wa kufikia kiunoni, lakini waliendelea kuokoa vilivyowezekana.
"Tukawa tunatoa vitu hapa, mwanangu akakimbilia kule kwake na yeye akitoa vitu kupeleka kwangu, tunafanya pilika hizo hadi maji yanafika ya kiuno tunaendelea kutoa vitu tulipomaliza tukatoka kwenda kukaa pale tunamsubiri hatma," anaeleza.
Athari katika kilimo
Kutokana na mafuriko hayo, matumaini ya ustawi wa mazao kutokana na shughuli za kilimo ambazo ndizo zinazotegemewa na wakazi wa Kijiji hicho yamepotea.
Kupotea kwa matumaini hayo, kunatokana na maeneo mengi ya ardhi ya kilimo kuingiwa na mchanga hivyo si bora tena kwa uzalishaji mazao, kama inavyoelezwa na Ofisa Kilimo wa Kijiji hicho, Zubery Utondwe.
"Maeneo yaliyopata mafuriko kwa sehemu kubwa yameletwa mchanga, yale maeneo ambayo watu walikuwa wanapanda mahindi, kunde na viazi, sasa mchanga ulioletwa hauwezi kustawisha mazao hayo," anasema.
Kwa mujibu wa Utondwe, jumla ya ekari 162 zimeathirika na mafuriko katika Kijiji hicho na kusababisha watu wapoteze mazao, ukiwemo mpunga, mtama, mihogo, migomba na hata minazi.
Kwa sasa anasema kinachopaswa kufanyika ni kuangalia mabonde yaliyobaki ili yatumike kuzalisha mazao hayo.
"Kwa harakaharaka tunapaswa tuangalie maeneo yaliyobakia hasa mabonde tunayoweza kupanda mazao hayo ya kiangazi ili kuwa na usalama wa chakula," anasema.
Katika kufanikisha hilo, ofisa kilimo huyo anapendekeza Serikali itoe msaada wa mbegu za muda mfupi kwa wanakijiji hao.
"Tunaiomba Serikali itupatie mbegu za muda mfupi ili tukawagawie wananchi wetu wakapambane kuotesha mazao na kupambana na hilo balaa la njaa linalokuja msimu ujao," anasema.
Ilichokisema Serikali ya Wilaya
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilwa, Yusuph Mwinyi anasema tayari wataalamu wa mazingira walishakwenda katika maeneo mbalimbali kutoa ushauri wa aina ya mbegu za mazao zinazohitajika.
Anaeleza huo ndiyo msaada ambao hata uongozi wa wilaya unaendelea kuuomba kwa wadau na Serikali kwa ajili ya wananchi.
"Msaada mwingine tunaouhitaji kwa ajili ya ustawi wa hawa watu kwa sasa maeneo yote yaliyoathiriwa, wananchi wanahitaji mbegu kama za maboga, mahindi na kunde," anasema.
Msingi wa kuhitajika kwa mbegu za mazao hayo, anasema ni uhalisia wa uwezo wa mazao hayo kuhimili ustawi katika ardhi yenye maji mengi.
"Na Serikali katika kulitambua hilo tumeshaanza kuleta mbegu lakini bado tunahitaji mbegu zaidi kutoka Serikali na wadau wengine," anaeleza.
Athari kwa Wilaya nzima
Mwinyi anasema mafuriko katika Wilaya ya Kilwa yameathiri Kata 14.
"Kata zilizoathirika ni Kikole, Kivinje Singino, Kwiteja, Tingi, Somanga, Mwitole, Mandawa, Kiranjeranje, Kinjumbi, Ukandawale, Mayuni, Songosongo, Kipatimu na Kibata," anasema.
Kutokana na mafuriko hayo, jumla ya kaya 1,020 zenye wanakaya 4,080 zimeathirika.
Anasema jumla ya nyumba 525 zimeharibika kwa baadhi ya maeneo na 495 zimeharibika kabisa na zinahitaji kujengwa upya.
"Nyumba nyingi kati ya hizi ni za udongo. Wananchi hawa baadhi yao walikuwa kwenye kambi tofauti zilizoandaliwa na Wilaya," anasema.
Kwa mujibu wa Mwinyi, jumla ya watu watano walipoteza maisha katika Wilaya hiyo, kati yao wanaume wanne na mwanamke mmoja.
"Vifo hivyo vilitokea katika maeneo tofauti, Kipatimu alifariki mmoja wa kike, Kijiji cha Namayuni alifariki mwananchi mmoja wa kiume, Miteja amefariki mmoja wa kiume, Kikole wananchi wawili wamefariki," anasema. |
Licha ya kukoma kwa mafuriko katika maeneo mbalimbali nchini, bado athari zake zinaendelea kuacha vi | Licha ya kukoma kwa mafuriko katika maeneo mbalimbali nchini, bado athari zake zinaendelea kuacha vilio na maumivu kwa wananchi wa maeneo yaliyokumbwa na majanga hayo katika siku za karibuni.
Mafuriko hayo yaliyotokana na mvua zilizoanza kunyesha tangu Oktoba mwaka jana, yameathiri maeneo mengi nchini na Kijiji cha Myumbu wilayani Kilwa katika Mkoa wa Lindi ni miongoni mwa vilivyoathirika.
Katika kijiji hicho, Kaya 207 zimeathirika kati ya 776 zinazounda Kijiji hicho cha Myumbu.
Matumaini ya uhakika wa kupata milo miwili hadi mitatu kwa siku waliyokuwa nayo wakazi wa Kijiji hicho, yameyeyuka.
Kwa mujibu wa wakazi wa Kijiji hicho, mafuriko zaidi yaliwakumba asubuhi ya Mei 4, mwaka huu, yakiambatana na Kimbunga Hidaya, kilichoanza Mei 2, mwaka huu.
Si mashamba, vyombo wala vyakula walivyokuwa wamehifadhi ndani vilivyopona, vyote vimesombwa na maji.
Matumaini ya maisha ya wengi baada ya athari hizo, ni misaada kutoka kwa wahisani na Serikali ambayo hata hivyo, upatikanaji wake ni kitendawili kisichoteguka.
Shuhuda za waathirika
Abdulrahman Kingoma ni miongoni mwa waathirika wa mafuriko katika Kijiji cha Myumbu wilayani Kilwa katika Mkoa wa Lindi.
Si nyumba, chakula wala vyombo alivyofanikiwa kuviokoa wakati wa mafuriko hayo, akisisitiza kila kitu kilisombwa na maji.
Kwa mujibu wa Kingoma, ndani ya nyumba yake hiyo, pamoja na kitanda, vyombo na mavazi, pia kulikuwa na gunia moja na nusu la mtama na mifugo.
"Nilikuwa na ghala la kuhifadhia mahindi na mtama na lilikuwa na mtama gunia moja na nusu limeondoka, banda la kuku limeondoka yaani sina chochote," anasema.
Hali hiyo, imemfanya Mzee Kingoma awe katika kile alichokiita ufukara uliopitiliza, kwani hata chakula akichotumaini kimfikishe wakati wa mavuno ya kilimo cha msimu huu hakipo tena.
"Maisha yangu yamekuwa magumu, mlo, mavazi hasahasa vyombo vya kupikia sina. Kwa hiyo wamenisaidia majirani tu kwamba kaa hapa na hadi sasa sijala vizuri," anasimulia.
Mwananchi limeshuhudia mabaki machache ya nyumba aliyokuwa akiishi Kingoma na kwamba namna inavyooneka sasa, ni vigumu kumwaminisha mtu kwamba eneo hilo lilikuwa na nyumba.
Hata hivyo, kuwa kwake hai kumetokana na alichoeleza kuwa, tukio hilo lilitokea mchana, ingekuwa usiku pengine asingekuwa hai.
Wakati wa tukio hilo kwa mujibu wa Kingoma, hata vijana anaoishi nao katika eneo hilo hawakuwepo nyumbani kila mmoja alikuwa matembezini.
Ni yeye na mkewe pekee ndiyo waliokuwa nyumbani wakati mafuriko yanatokea.
Baada ya hali hiyo, anasema aliondoka katika eneo hilo kuhamia kwa majirani, eneo ambalo angalau ni vigumu kufikiwa na maji.
Wakati unastaajabu yaliyomtokea Kingoma, yaliyomsibu Darlin Ngalamba (83) yatakushangaza.
Mjane huyo anayeishi na wajukuu zake wanne katika nyumba yake ya udongo kando ya mto wenza, shughuli za kilimo ndiyo nguzo ya maisha yake.
Ingawa hatma ya chakula na mahitaji yake mengine yanatokana na shughuli za kilimo, ufungaji kuku nao ni sehemu ya maisha yake.
Kutokana na mafuriko hayo, ni kuku wawili kati ya 30 ndiyo aliofanikiwa kuwaokoa, hivyo matumaini ya ufungaji ni kama yamepotea.
Kama hiyo haitoshi, mjane huyo aliyekuwa na ekari tano zilizostawi mihogo na migomba kwa sasa imebaki hadithi, kwani hakuna ndizi wala muhogo uliobaki shambani hapo, yote yameondoshwa na mafuriko.
"Migomba imedondoka, mihogo na kuku baada ya hapo ndiyo tukafanya utaratibu wa kununua wengine," anasema.
Hali hiyo imebadili mtindo wa maisha yake kutoka kujitegemea na wajukuu zake, hadi kugeukia misaada ya wasamaria wema.
Kukosa kwake mazao na vingine vingi, kumefanya awe na mlo wa wasiwasi, kwa kuwa hana uhakika wa kupata kila siku.
"Vitu vimeondoka ulaji umekuwa wa tabu, tangu tumeamka asubuhi hatujajua lolote kwa sasa, tuhangaike hangaike mtu ukipata robo umeletewa ukala maisha yanaendelea," anasema.
Kwa umri alionao ni vigumu kumuona tena shambani na hata hivyo, analalamikia maumivu ya miguu kwa kile anachodai ni ugonjwa wa utu uzima.
Kinachofanyika ni mjukuu wake mwenye umri wa miaka 25, kufanya vibarua katika mashamba ya Kijiji cha jirani ili kuisaidia familia walau kupata mlo.
Ilivyotokea
"Tuliamka na mvua ilianza kunyesha kidogokidogo, mvua iliendelea hadi saa tatu asubuhi maji yanaanza kufurika. Wajukuu zangu wakanambia kuna maji," anasema.
Kutokana na umri wake, ilikuwa vigumu kwa Darlin kutembea mwenyewe hadi maeneo yaliyokuwa salama, ukifika wakati juhudi zake zilikoma.
Katika hali hiyo, anasema walitokea wasamaria wema waliomsaidia mjukuu wake mkubwa kumbeba hadi katika eneo lisilokuwa na maji.
Kwa mujibu wa Darlin ilimchukua wiki moja kuishi nje ya nyumba yake, akisubiri maji yaondoke na baadaye akirejea.
"Kurudi hapa vitu vyote hamna, mabeseni, sufuria naletewa na watu kama msaada," anasema.
Kutokana na hali hiyo, anasema angetamani kupata msaada kutoka serikalini hasa wa chakula kwa hatua za haraka kwa kuwa ndicho kitu muhimu katika uhai.
"Serikali itusaidie tuliopatwa na matatizo, tunahitaji msaada wowote, kwa wakati huu vyakula kwa sababu hatuna pa kupikia mengine yatazidi kuendelea na Serikali," anaeleza.
Misaada kizungumkuti
Licha ya Darline na Kingoma kuweka matumaini yao kwa Serikali kuwasaidia, msaada uliofikishwa katika eneo hilo kutoka serikalini, unatosha mlo mmoja kwa siku pekee.
Hata hivyo, si waathirika wote 273 wa mafuriko katika Kijiji hicho watafikiwa na msaada huo, bali ni watu 80 pekee kutokana na uchache wa msaada huo.
Rabii Mbonde ni mmoja wa wajumbe wa Kamati ya maafa ngazi ya Kijiji, anayesema msaada waliopokea haukidhi idadi ya waathirika wote.
"Tumeletewa msaada tunapaswa kuwagawia watu 80 ndani ya Kijiji chetu lakini waathirika tunao zaidi ya 300, kwa hiyo tunashindwa namna ya kuugawanya," anasema.
Hali hiyo kwa mujibu wa Rabii, imesababisha manung'uniko kutoka kwa baadhi ya wananchi wakidhani viongozi wa Serikali wameficha baadhi ya misaada.
"Kilichotokea sasa wananchi wanalalamika, wanazungumza mengi kwa kwanini hawa wapate kwanini hawa wakose tunaomba msaada zaidi," anasema.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Hamidu Mnola anasema msaada waliopokea ni kilo 100 za unga, 400 za maharage, blanketi 100, vyandarua 130 na ndoo za kuwekea maji.
Pamoja na unga na maharage, anasema katika Kijiji hicho, wamepokea magodoro sita kwa ajili ya kuwapatia waathirika.
Misaada imekuja kwa kiwango hicho, ilhali Kaya zilizoathirika ni 207 kati ya 776 zilizopo katika Kijiji hicho, kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo. |
Nafuu ya kodi, ushuru na tozo katika huduma za mawasiliano, kupungua kwa gharama ya data na kuimaris | Nafuu ya kodi, ushuru na tozo katika huduma za mawasiliano, kupungua kwa gharama ya data na kuimarishwa kwa elimu ya Tehama na Akili Bandia ni miongoni mwa matarajio ya wadau kuhusu sekta ya mawasiliano kuelekea Bajeti Kuu ya Serikali.
Matarajio ya wadau hao, wakiwemo wanazuoni yanakuja wakati Juni 13, mwaka huu Serikali ikitarajia kusoma bajeti yake kuu bungeni jijini Dodoma.
Bajeti hiyo inahusisha mipango ya kifedha ya uendeshaji wa Serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/25.
Kwa mujibu wa wadau hao, suala la nafuu ya kodi, ushuru na tozo katika huduma za mawasiliano wanatarajia liwepo ndani ya bajeti hiyo, wakisema litarahisisha huduma hizo.
Sambamba na nafuu hiyo, wanatarajia kupungua kwa gharama za mawasiliano na kuanzishwa elimu katika masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) na akili bandia ili kuimarisha udhibiti wa mifumo nchini.
Katika mazungumzo yao na Mwananchi kwa nyakati tofauti, wadau hao wanapendekeza baadhi ya tozo zipunguzwe ili kuvutia uwekezaji katika sekta ya mawasiliano.
Kwa upande wa kampuni ya huduma za mawasiliano ya Tigo Tanzania, inatarajia bajeti hiyo itakuja na ahueni ya mambo manne inayoyataja kuwa kikwazo cha biashara hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Kodi wa kampuni hiyo, Francis Temba anayataja mambo hayo ni kupunguzwa kwa asilimia 17 ya ushuru wa bidhaa za huduma ya mawasiliano kielektroniki.
Kwa sababu kiwango hicho cha ushuru ni kikubwa na kinaongeza gharama za utoaji huduma, Temba anapendekeza bajeti hiyo ije na punguzo hadi kufikia angalau asilimia 10.
"Ushuru huu ndiyo unaoongeza gharama kwenye huduma za mawasiliano, ukipungua gharama za mawasiliano zitakuwa nafuu na hivyo kurahisisha kila mtu kunufaika nazo," anasema.
Sambamba na ushuru huo, Temba anapendekeza bajeti hiyo ije na msamaha au ifuate kabisa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye ununuzi wa simujanja.
Mbobezi huyo wa masuala ya kodi katika kampuni ya Tigo, anasema kwa sasa mfanyabiashara anaponunua simujanja anatozwa asilimia 18 ya VAT bandarini.
So hivyo tu, anasema mfanyabiashara huyo huyo anapaswa kulipa tena VAT kwa asilimia 18 kila anapouza simujanja.
Hayo yanafanyika ilhali Tanzania na dunia kwa sasa imeelekeza juhudi katika matumizi ya intaneti ili kunufaika na uchumi wa kidigitali, kwa mujibu wa Temba.
"Hii maana yake unafanya simujanja ziendelee kuwa ghali na hivyo watu wachache ndiyo wawe na uwezo wa kuzimiliki, wakati wengine washindwe. Hii inaturudisha nyuma," anaeleza.
Katika maelezo yake, Temba anatarajia mabadiliko katika utaratibu wa ulipaji wa ushuru wa mabango kutoka kwa manispaa hadi kutafutwa mamlaka moja itakayozikusanya zote.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, kampuni kama za mawasiliano aghalabu huwa na mabango karibu nchi nzima, kwenye ushuru wanalazimika kuhangaika na wahasibu zaidi ya 100 wa manispaa zote nchini, jambo alilodai ni usumbufu.
"Kungekuwa na mamlaka moja inayokusanya ushuru wote na inaugawanya kwa manispaa ingeturahisishia. Kuna wakati Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilikuwa inakusanya lakini mwaka jana ikarudishwa kwa manispaa," anasema.
Matarajio mengine kwa mujibu wa Temba, ni kuondolewa kwa ushuru wa Access kwa kampuni zinazodhibitiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
"Sheria iliyopo sasa inalazimu ushuru huo ulipwe mara mbili, kwa mfano Tigo anauza intaneti kwa jumla kwa kampuni nyingine yeye (Tigo) anatozwa hiyo Access duty.
"Huyu aliyeuziwa naye akienda kuuza TRA inambana alipe ushuru huo kwa hiyo kuna utozaji mara mbilj hapo," anasema.
Anasisitiza mapendekezo ya watoa huduma za mawasiliano ni kuhakikisha ushuru huo unatozwa mara moja pekee.
Mwanazuoni aliyebobea katika sekta ya mawasiliano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Mussa Kissaka anatarajia bajeti hiyo ije na mpango mahsusi wa kupunguza gharama za mawasiliano.
Kwa mtazamo wa Dk Kissaka, gharama hizo zinapaswa kuendana na uhalisia wa kipato cha mtanzania, zisifananishwe na ilivyo katika mataifa mengine.
Kupungua kwa gharama hizo, alitaka kuambatane na kuimarishwa kwa mifumo ya data ili kuboresha huduma iwe na kasi inayoridhisha.
“Sio unafungua tovuti nusu saa bado haijafunguka, au linatokea tatizo tunakosa huduma ya intaneti ukiuliza unaambiwa sababu umeme na mambo mengine, haya natarajia yataboreshwa,” alisema.
Matarajio yake mengine ni kupungua kwa gharama inayotozwa na Serikali kuziuzia kampuni zinazotoa huduma za mawasiliano, ili kuvutia wawekezaji wengi kuleta mifumo yao nchini.
Mhadhiri mwingine aliyebobea katika mawasiliano na kompyuta, Dk Hadija Mbembati anasema bajeti hiyo ijikite katika uelimishaji wa vijana.
Elimu hiyo kwa vijana, anasema ijikite katika masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), ili kuwajengea ubobevu kwa kuwa ndiko Dunia inakoelekea.
“Serikali ijikite kutoa mafunzo ya vitendo kwa vijana na bahati nzuri nimesikia kuna mchakato wa kuanzisha chuo cha Tehama Dodoma kikianza kitakuwa na matokeo mazuri,” anasema.
Msingi wa hoja yake hiyo ni kile alichoeleza, licha ya Tanzania kuwa na mifumo mbalimbali, kumeshuhudiwa changamoto za usalama katika mifumo hiyo.
Anasema uwepo wa vijana waliobobea kwenye eneo hilo, watasaidia kudhibiti mifumo hiyo isichezewe au kuingiliwa kwa namna yoyote.
Sambamba na Tehama, anatarajia bajeti hiyo ije na mpango mahsusi wa uelimishaji vijana kuhusu teknolojia ya akili bandia, akisisitiza ndiko dunia inakoelekea.
“Umuhimu wa kuwaelimisha vijana wabobee katika AI unatokana na mwenendo wa dunia kwa sasa. Dunia inaelekea kwenye mabadiliko makubwa ya teknolojia inabidi vijana waendane nayo,” alisema. |
Ni kipindi cha wakazi wa Kigamboni kufunga mkanda, kauli hiyo inaakisi uhalisia wa uvumilivu wa zaid | Ni kipindi cha wakazi wa Kigamboni kufunga mkanda, kauli hiyo inaakisi uhalisia wa uvumilivu wa zaidi ya mwaka wanaopaswa kuwa nao watumiaji wa vivuko katika eneo la Kigamboni-Magogoni.
Wanachopaswa kuvumilia hasa ni huduma hafifu katika eneo hilo kwa kipindi cha karibu mwaka, zitakazosababishwa na uchache wa vivuko, baada ya vikubwa vilivyokuwepo kupelekwa kwenye matengenezo makubwa.
Matarajio ya hali ngumu ya huduma katika eneo hilo, yanatokana na vivuko vya MV Magogoni na MV Kigamboni kuwa nje ya huduma kutokana na matengenezo makubwa.
Juni 6, mwaka huu Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (Temesa), ilitangaza kusimamisha huduma za kivuko cha MV Kigamboni kutokana na kwenda kufanyiwa matengenezo makubwa.
Kabla ya kivuko hicho, kivuko cha MV Magogoni hakikuwa katika huduma tangu Februari mwaka 2023, kilipopelekwa Mombasa nchini Kenya, kwa ajili ya matengenezo makubwa.
Kipindi cha kufunga mkanda
Kutokana na matengenezo ya kivuko cha MV Kigamboni, wananchi wanaotumia huduma ya kivuko hicho, watalazimika kufunga mkanda kwa takriban mwaka.
Makadirio ya muda huo, yanatokana na kile kilichoelezwa na Meneja wa Vivuko Temesa Kanda ya Mashariki, Abdulrahman Ameir kuwa, bado zabuni haijatangazwa.
Kinachofanyika sasa, alieleza ni hatua za manunuzi zinazohusisha tathmini ya kujua kitu gani cha kubadilishwa na kitagharimu kiasi gani cha fedha kwenye kivuko hicho.
“Mchakato wa manunuzi utafanyika kwa wiki mbili na ukimalizika ndipo tutakapojua kitu gani kinahitajika na zabuni itatangazwa ili kumpata mzabuni atakayekuwa na uwezo wa kufanya matengenezo yatakayobainika,” alieleza.
Baada ya mchakato wa manunuzi kwa mujibu wa Ameir, zabuni itatangazwa kimataifa ambayo kisheria itakuwa kwa siku zisizozidi 21 hadi atakapopatikana mkandarasi.
Meneja huyo alifafanua mchakato huo utafanikisha kupatikana mkandarasi na kuanzia hapo ndipo kazi ya matengenezo itakapoanza, ikihusisha kubadilisha injini zote nne, gear box, mifumo ya uendeshaji na mabati.
Kwa uzoefu wa Ameir, alisema kazi hiyo itachukua si chini ya miezi nane, kwa kuwa ndani yake kuna mchakato wa mkandarasi kuagiza injini, jambo ambalo aghalabu huchukua muda mrefu.
“Kwenye kuagiza injini huwa inachukua muda mrefu kwa sababu ni zote nne, kwa hiyo hapa mkandarasi kwa kawaida hutumia muda mrefu,” alisema.
Kutokana na maelezo ya meneja huyo, watumiaji wa kivuko hicho watalazimika kufunga mkanda muda wote huo wakisubiri kukamilika kwa ukarabati huo.
Subira kama hiyo, wanapaswa kuwa nayo kwa kivuko cha MV Magogoni ambacho Naibu Waziri wa Ujenzi, Geofrey Kasekenya aliahidi kitakamilika Desemba mwaka huu.
Kivuko hicho kilichopaswa kukamilika Agosti mwaka jana, sababu za kuchelewa kwake ni kile kilichobainishwa katika uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kuwa, Serikali ilichelewa kumlipa mkandarasi kwa ajili ya kukamilisha kazi.
Malipo ya awali yaani asilimia 10 ya Sh7.5 bilioni ambayo Serikali ilipaswa kumlipa mkandarasi African Marine and General Engineering Company Ltd Februari mwaka jana, ndiyo kwanza imeyafanya Februari mwaka huu.
Hata hivyo, bado hadi jana Serikali haikuwa imekamilisha malipo yaliyosalia kwa ajili ya matengenezo ya kivuko hicho, hivyo bado kunaibuka mashaka katika matumaini ya kurejea.
Mapito ya kufunga mkanda
Katika kipindi cha kufunga mkanda, watumiaji wa vivuko hivyo watatumia muda mrefu kupata huduma katika eneo la Kigamboni-Magogoni.
Vivuko vinavyoendelea kutoa huduma kwa sasa ni MV Kazi na Sea Tax mbili.
Uwezo wa MV Kazi ni kupakia jumla ya abiria 800 na magari madogo 11 kwa wakati mmoja, huku kila Sea Tax moja ikiwa na uwezo wa kupakia abiria 250 kwa safari moja.
Kwa maneno mengine safari moja ya vivuko vyote vinavyoendelea na huduma sasa, vitabeba jumla ya abiria 1,300.
Hata hivyo, katika vivuko hivyo MV Kazi inafanya kazi kwa saa 24, huku Sea Tax zikifanya kazi kwa saa nane pekee, kwa mujibu wa mkataba wake wa ukodishaji kati ya Temesa na Kampuni ya Azam Marine Ltd.
Vivuko vina uwezo huo, ilhali uhalisia wa mahitaji ya huduma ya kuvuka kwa siku ni takriban watu 60,000 wanaokadiriwa kuvuka kila siku.
Kutokana na mahitaji hayo vivuko vyote kwa pamoja, ili kukidhi haja ya abiria wote 60,000 wanaokadiriwa kuvuka, vinapaswa kufanya safari 46 kwa siku.
Mashaka kwenye bajeti
Ingawa wakazi hao wanakadiriwa kufunga mkanda kwa takriban mwaka hadi vitakaporejea MV Magogoni na Kigamboni, lakini yapo mambo yanayoibua mashaka ya kukamilika kwa kazi hizo haraka.
Ukiachana na michakato iliyoelezwa na Ameir kuhusu matengenezo, masuala ya kibajeti huenda yakasababisha MV Kigamboni nayo ikakwama kama ilivyotokea kwa MV Magogoni.
Hilo linatokana na uhalisia kwamba, Ameir alisema bajeti ya matengenezo ya MV Kigamboni itatokana na fedha iliyotengwa kwa ajili ya matengenezo ya vivuvo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25.
Katika bajeti hiyo, Wizara ya Ujenzi imetenga Sh11.535 bilioni kwa ajili ya matengenezo ya vivuko mbalimbali, kikiwemo Kigamboni na Magogoni.
Katika fedha hiyo, MV Magogoni inapaswa kulipiwa Sh6.7 bilioni kama gharama za kukamilisha matengenezo, huku MV Kigamboni ikikadiriwa kuhitaji takriban Sh6 bilioni kwa ajili ya matengenezo.
Kwa maneno mengine, inahitajika Sh12 bilioni kukamilisha malipo ya MV Magogoni na kufanikisha matengenezo makubwa ya MV Kigamboni, fedha ambayo ni zaidi ya ile iliyotengwa katika bajeti.
Mbali na hilo, kwenye Sh11.535 bilioni iliyotengwa ndani ya bajeti hiyo ya Wizara ya Ujenzi kwa ajili ya matengenezo ya vivuko hivyo, hiyo hiyo inapaswa kugharimia matengenezo ya MV Mara, MV Ujenzi, MV Kome II, MV Misungwi, MV Nyerere na MV Kyanyabasa.
Vingine ni MV Kitunda, MV Lindi, MV Kazi, MV Mwanza, MV Ukara I, MV Ukara II, MV Sabasaba, MV Pangani II pamoja na ukarabati wa MV Kilombero II kabla ya kukihamishia eneo la Mlimba – Malinyi.
Vilevile, ukarabati wa boti ya uokozi ya MV SAR III, ukarabati wa kivuko MV Malagarasi na MV Mafanikio pamoja na ufuatiliaji na tathmini ya miradi hiyo.
Gharama kwa wananchi
Kupungua kwa vivuko hivyo kutawagharimu baadhi ya wananchi ambao awali walitumia kuvuka kutoka Kigamboni hadi Magogoni kwa Sh200, lakini sasa baadhi watapaswa kuzunguka kwa daladala kwa gharama ya Sh700.
Kwa upande wa wenye magari wanaotokea Kigamboni, ili kuwahi Posta watapaswa kuzunguka kwa njia ya Daraja la Nyerere njia ambayo kimsingi ni ndefu na inagharimu mafuta.
Hata hivyo, kipindi hicho cha changamoto ya usafiri wa vivuko ni fursa ya kuongezeka kwa mapato ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Ongezeko la mapato hayo, litatokana na kuongezeka kwa magari yatakayopita katika daraja la Nyerere ambao hulipia Sh3,000 kwa gari ndogo na Sh200 kwa pikipiki. |
Licha ya Wizara ya Ardhi kupiga marufuku uuzaji wa ardhi kupitia kampuni za madalali zenye mabango k | Licha ya Wizara ya Ardhi kupiga marufuku uuzaji wa ardhi kupitia kampuni za madalali zenye mabango katika maeneo mbalimbali nchini, wadau wamesema hatua hiyo haitakuwa muarobaini wa utapeli na migogoro katika sekta ya ardhi.
Marufuku ya uuzaji wa ardhi kupitia kampuni hizo za udalali, ilitolewa juzi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa alipokuwa akisikiliza kero za wananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Katika marufuku hiyo, Silaa alitaka badala ya kuwepo kwa utitiri wa mabango ya kampuni hizo, yeyote anayetaka kuuza ardhi apeleke taarifa katika Ofisi ya Ardhi ya Halmashauri husika.
“Na wananchi wajue kwamba viwanja nchi hii vya watu binafsi vya kampuni binafsi vinauzwa ofisi ya ardhi ya Wilaya,” alisisitiza huku akitoa siku saba mabango yote yaondolewe.
Msingi wa maelekezo hayo ya Silaa ni kukithiri kwa migogoro ya ardhi inayosababishwa na uholela katika biashara hiyo.
Ingawa Serikali imependekeza hivyo, wadau wa ardhi wana mtazamo kinzani, wakisema marufuku ya mabango hayo haitakuwa muarobaini wa migogoro ya ardhi.
Kwa mujibu wa wadau hao, kukoma kwa migogoro hiyo kutatokana na wananchi kuwa na elimu ya kutosha kuhusu biashara ya ardhi, Serikali udhibiti uholela katika biashara hiyo na ardhi iliyopo irasimishwe.
Udhibiti wa biashara
Akizungumzia hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Haki Ardhi, Cathbert Tomitho alisema badala ya marufuku iliyotolewa na Silaa, alipaswa aje na mfumo bora wa udhibiti wa biashara ya ardhi.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, biashara ya rasilimali hiyo kwa sasa inafanyika kiholela na ndiyo sababu ya mianya ya migogoro na utapeli.
“Katazo hilo lingekuwa na mantiki kama lingesimamisha biashara ya ardhi na kusubiri kuwekwa utaratibu wa usimamizi wa biashara hiyo,” alisema.
Katika msisitizo wa hoja yake hiyo, Tomitho alisema haoni katazo hilo likifua dafu, akidokea kuna uwezekano kampuni hizo zikaacha mabango na kuhamia kufanya biashara hiyo kupitia mitandao ya kijamii.
“Soko la ardhi halijadhibitiwa, kila kampuni inayopima viwanja inauza bei yake, manispaa inanunua bei yake, watu binafsi wananunua kwa bei yao. Kuondoa vibao hakuondoi migogoro,” alisisitiza.
Kilichozungumzwa na waziri huyo kwa mujibu wa Tomitho, ni utashi wake binafsi kwani hata sheria ya ardhi ya mwaka 1999 inaruhusu kupima na kuuza viwanja, akisema nayo iko holela.
“Natamani matamko ya Waziri yakabadilishe sera na sheria, kwa kuwa pamoja na nia njema aliyonayo lakini sheria haimpi nguvu ya kutekeleza anachokitaka,” alisema.
Hata hivyo, alieleza kinachowafanya wananchi waendelee kuziamini kampuni hizo za udalali ni hatua yake ya kusikika katika vyombo vinavyoaminika vya habari.
Urasimishaji ardhi
Mwanazuoni wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Dk Emmanuel Mchome alisema ili kukabili migogoro ya ardhi inayosababishwa na biashara katika sekta hiyo, ni muhimu kutambua umiliki.
Utambuzi wa umiliki wa ardhi, alisema ufanyike wakati wa upimaji na ramani itakayopatikana inapaswa kubandikwa kwenye ofisi ya Kijiji au Kitongoji kwa miezi mitatu.
Kwa mujibu wa Dk Mchome, ramani hiyo inapaswa kuwa na majina ya wamiliki wa kila ardhi na ukubwa wa eneo wanalolimiliki.
“Kwa kipindi cha miezi hiyo mitatu, kila mmoja atakwenda kuangalia jina lake na ardhi yake, kama atatokea Mwananchi mwenye pingamizi atasema na utawekwa utaratibu wa kusikiliza na kutatua,” alisema.
Alieleza hiyo itasaidia kujua wamiliki halali wa maeneo na hivyo kuepusha utapeli na uuzaji holela wa ardhi.
Mbali na mapendekezo yake hayo, alieleza kumekuwa na utapeli kwenye biashara ya ardhi na hasa unafanyika kwa watu kuuza maeneo ilhali hawayamiliki.
Alikwenda mbali zaidi na kueleza wapo waliowahi kulipwa fidia wakati wa utekelezwaji wa miradi ya Serikali ilhali si wamiliki halali wa maeneo husika.
“Hii iliwahi kutokea Bagamoyo kwenye mradi mmoja hivi, hatimaye wakati Serikali inataka kuanza kutekeleza mradi mmiliki halali anajitokeza kwa hiyo imechelewesha kazi kuendelea,” alisema.
Kampuni za udalali zinasemaje
Madalali nao wanasisitiza umuhimu wa elimu kuhusu biashara ya ardhi kwa wananchi kama msingi wa kupunguza migogoro inayojitokeza, badala ya kupiga marufuku mabango pekee kama anavyoeleza Albert Saanane kutoka Kampuni ya EPL property.
Saanane alisema kwa mtazamo wake wananchi wengi wamekosa taarifa sahihi za wapi wauze au wanunue viwanja ndiyo maana migogoro na utapeli hutokea.
“Biashara ya uuzaji viwanja kupitia kampuni inaonekana ngeni miongoni mwa watu wengi ukiangalia watu walikuwa wamezoea kuuza na kununua kiholela mitaani, sasa hatua ya Waziri kupiga marufuku itawashtua watu ni wapi wakanunue viwanja na zile kampuni zitashindwa kutekeleza janjajanja zao,” alisema.
Kwa mtazamo wa Saanane, marufuku ya Silaa haitafua dafu katika kukomesha migogoro inayotokana na uuzwaji holela wa viwanja, akisisitiza itachukua muda kwa jambo hilo kufanikiwa.
Lakini dalali huyo, alikiri marufuku hiyo itasaidia kupunguza migogoro, akipendekeza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kwa ukubwa ili wapate uelewa wa biashara hiyo.
“Kwa kuwa itapaswa kuuzia halmashauri kuna baadhi ya kampuni ambazo hazijakamilika hazitakwenda hivyo ni hatua nzuri kinachotakiwa kampuni zifuate utaratibu ili mambo yawe yamenyooka,” alisema Saanane.
Serikali za mitaa
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Serikali za mitaa jijini Dar es Salaam, Juma Mwingamno alisema kitendo hicho kitaepusha migogoro ya wawekezaji kwenye ardhi.
“Busara za Waziri ni sahihi kwa kuwa kampuni husika inayouza viwanja kwa watu ikienda kufanya jambo hilo chini ya usimamizi wa halmashauri ina maana mwekezaji katika ardhi hiyo atapata sehemu sahihi na ni rahisi kukwepa watu wasio waaminifu,” alisema.
Sambamba na kuunga mkono katazo la Silaa, Mwenyekiti huyo aligusia uhalali wa mamlaka ya viongozi wa Serikali za Mitaa katika biashara ya ardhi, akisema sheria haiwatambui.
Badala yake, alisema wajibu wa viongozi hao ni kuwatambua wakazi wa maeneo husika.
“Wanachopaswa kujua ni nyumba namba fulani ni ya mtu fulani wanaoishi ni kinanani. Mtu anapokuja kubadilisha umiliki sisi wajibu wetu ni kutoa taarifa kwa anayetakiwa kusimamia taratibu za mauziano.
“Wanasheria au Mahakama kwasababu hawajui jengo wala wenyewe hivyo sisi hatuna dhamana ya kusimamia mauzo,” alibainisha.
RCs waeleza sababu za migogoro
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu alisema katika eneo analoliongoza migogoro ya ardhi aghalabu husababishwa na uvamizi wa maeneo yaliyotengwa.
“Unakuta mtu amevamia eneo la Serikali ambalo lilitengwa kwa ajili ya shughuli fulani, hapa ndipo migogoro hutokea,” alisema.
Sababu nyingine, alisema ni mtu na mtu kuvuka mpaka uliowekwa na mamlaka wakati inamilikisha ardhi, kadhalika ipo migogoro ya ukoo au familia.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Abas Ahmed Abas alisema kukosekana kwa umilikishwaji ni sababu mojawapo.
“Mtu anaamini anamiliki sehemu lakini kisheria haionekani kama yeye ndiye anayemiliki. Kitendo hiki kinarahisisha tapeli kujitokeza akishajua hilo,” alisema.
Lakini kukosekana kwa elimu, alisema kunasababisha watu wasijue haki zao kwenye ardhi zao na hilo ndilo linalosababisha watu wanunue maeneo yasiyostahili. |
Baada ya kivuko cha MV Kigamboni kupitiliza muda wa matengenezo makubwa kwa zaidi ya mwaka sasa, hat | Baada ya kivuko cha MV Kigamboni kupitiliza muda wa matengenezo makubwa kwa zaidi ya mwaka sasa, hatimaye Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (Temesa), imetangaza kukipeleka katika matengenezo hayo.
Uamuzi huo wa Temesa unakuja ikiwa imepita wiki moja, tangu gazeti la Mwananchi lichapishe mfululizo wa ripoti maalum kuhusu kucheleweshwa kwa matengenezo ya baadhi ya vivuko vinavyoendeshwa na wakala huo.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kivuko cha MV Kigamboni kilipaswa kupelekwa kwenye matengenezo makubwa mwanzoni mwa mwaka 2023, lakini kilipitiliza muda huo bila hilo kufanyika.
Hali yake ilikuwa mbaya zaidi hadi ikasababisha Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (Tasac), ikisimamishe kutoa huduma ya uvushaji abiria kulinda usalama wao, lakini bado kiliendelea kutoa huduma hiyo.
Katika ripoti hiyo iliyochapishwa kuanzia Mei 27, mwaka huu, ilieleza kitendo hicho kinakiuka Sheria ya Usalama wa Vyombo vya Majini (SOLAS) ya mwaka 1974 inayotaka chombo kinachotoa huduma katika maji ya bahari kifanyiwe ukarabati mkubwa kila baada ya miaka mitano.
Sambamba na kukiukwa kwa sheria hiyo, pia kitendo hicho kinakiuka masharti ya kitaalamu ya usalama wa vivuko (Sea Worthness) inayotaka Injini za vivuko hivyo kubadilishwa mara tu zitakapofanya kazi kwa saa 10,000.
Taarifa ya kusitisha
Juni 6, mwaka huu Temesa kupitia kitengo chake cha Masoko na Uhusiano, ilitangaza kusitisha huduma za kivuko hicho kuanzia Juni 7, ikieleza kinakwenda kufanyiwa ukarabati mkubwa.
Katika taarifa hiyo, Temesa iliweka wazi huduma za uvushaji abiria katika eneo la Magogoni-Kivukoni, zitaendelea kutolewa na Kivuko cha MV Kazi na Sea Tax.
Aidha, wenye magari walitakiwa kutumia njia mbadala kupitia Daraja la Mwalimu Nyerere ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza kutokana na MV Kigamboni kutokuwepo.
"Shughuli za uvushaji katika eneo hilo, zitaendelea kutolewa kama kawaida kwa kutumia kivuko cha MV Kazi na Sea Tax," imeeleza taarifa hiyo.
Hata hivyo, taarifa hiyo ya Temesa haikuweka wazi kwamba ni lini hasa kivuko hicho kitapelekwa, wapi na lini kitarejea kuendelea na huduma.
Hali ilivyokuwa
Baada ya wakala huo kusitisha huduma za kivuko hicho, Mwananchi liliweka kambi katika eneo la Magogoni-Kivukoni kwa saa nane kuanzia asubuhi na kujionea uhalisia wa huduma zilivyokuwa.
Katika eneo hilo tangu asubuhi hadi mwandishi wa habari hii anaondoka saa 6:13 mchana, ni kivuko kimoja tu cha MV Kazi ndicho kilichokuwa kinatoa huduma.
Hakukuwa na Sea Tax kama ilivyotangazwa katika taarifa ya Temesa, badala yake kivuko hicho cha Kampuni ya Azam Marine Ltd kiliegeshwa pembezoni mwa bahari kama kinakarabatiwa.
Kivuko hicho kiliegeshwa upande wa Magogoni (Posta), si mbali sana na kilipoegeshwa kivuko cha MV Kigamboni kinachotarajiwa kupelekwa kwenye ukarabati mkubwa.
Kutokana na huduma kutolewa na kivuko kimoja, kulishuhudiwa changamoto ya usafiri na abiria walilazimika kusubiri kwa saa moja hadi zaidi ili wahudumiwe.
Idadi kubwa ya abiria ilishuhudiwa upande wa Kivukoni (ilipo Wilaya ya Kigamboni), wakisubiri huduma ya kuvushwa kwenda upande wa Posta.
Hiyo inatokana na kile kilichoelezwa na baadhi ya abiria kuwa, muda wa asubuhi watu wengi wanakwenda Posta yalipo maeneo yao ya kazi.
Kwa mujibu wa abiria hao, wengine wanakwenda lilipo soko la samaki Ferry kwa ajili ya kulangua bidhaa, ndiyo sababu abiria wengi kwa muda wa asubuhi huwa upande wa Kivukoni.
Wazoefu hao wa huduma ya usafiri huo, wanasema jioni mambo hubadilika, kwani abiria wengi huwa upande wa Magogoni kwa kuwa wanatoka kazini kurudi nyumbani Kigamboni.
Malalamiko ya abiria
Hali imekuwa ngumu kwa Mariam Hemed anayehudumiwa na vivuko hivyo, kwa kile alichoeleza hatua ya kubaki kivuko kimoja imesababisha wasubiri muda mrefu hadi kupata huduma.
Kwa mujibu wa Mariam anayefanya biashara ya samaki Mjimwema, alifika katika eneo hilo saa 3 asubuhi lakini amefanikiwa kuvuka saa 4.
Hayo yote yametokea kwa sababu ya kile alichoeleza, kivuko kinachotoa huduma ni kimoja ambacho kiuhalisia kinazidiwa mahitaji.
"Usafiri tabu kuna kivuko kimoja tu, tunakaa saa nzima kusubiri kivuko nimefika saa 3 nimevuka saa 4, hali mbaya," alisema.
Aziz Radhi yeye alijikuta anachelewa kufika kazini alikopaswa kufika saa 2 asubuhi, lakini hadi saa 3 alikuwa Kigamboni.
Yote hayo kwa mujibu wa Radhi, ni matokeo ya kuwepo kwa kivuko kimoja kinachotoa huduma katika eneo hilo, akisisitiza umuhimu wa kuharakishwa ukarabati wa MV Kigamboni na Magogoni.
"Zile Sea Tax leo hakuna kabisa lipo kivuko kimoja hali imekuwa mbaya, basi wangeweka zile Sea Tax zingesaidia," alisema.
Simon Dalali abiria mwingine wa vivuko hivyo, alisema taarifa ya kufanyiwa ukarabati kwa kivuko hicho imemfurahisha.
"Najua hizi ni shida za muda mfupi tu kikitengenezwa kile kivuko mambo yatakuwa mazuri, lakini Serikali nayo ihakikishe inakamilisha mapema," alisema.
Hata magari ambayo Temesa ilishauri yapitie Daraja la Mwalimu Nyerere, baadhi yalishuhudiwa yakivushwa na baadhi ya madereva walipoulizwa walidai hawakuwa na taarifa.
"Mimi sikuona taarifa hiyo, ndiyo maana nimekuja hapa sio mbaya wakati mwingine sitapita tena nitatumia njia iliyoshauriwa," alisema Mic Michael.
Boti za wavuvi zatumika
Kutokana na uchache wa vivuko, baadhi ya abiria walishuhudiwa wakipanda boti za wavuvi kuvushwa kutoka upande mmoja kwenda mwingine.
Kupitia boti hizo, kila abiria hutozwa Sh1,000 kwa huduma ya kuvushwa na hata hivyo wanadai wanatumia muda mchache kuliko kusubiri kivuko cha MV Kazi pekee.
Noel Stephen alisema ni wanaume pekee ndiyo wanaweza kuvuka kwa boti hizo za wavuvi, lakini wanawake wanalazimika kusubiri MV Kazi kwa hofu ya usalama.
"Sisi hatujui kuhusu masuala ya sheria, mimi naangalia uharaka wa kufika ninapoenda. Kama wanataka masuala ya sheria waboreshe huduma zao," alisema.
Ni kinyume cha sheria
Hata hivyo, uvushaji wa abiria kwa kutumia boti hizo za wavuvi ni kinyume cha sheria ya huduma za vivuko, kama inavyoelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tasac, Mohamed Salum.
Uharamu wake unatokana na kile alichoeleza, boti hizo hazijapewa vibali vya kuvusha abiria hivyo zinatekeleza jukumu hilo kinyune na utaratibu.
Sambamba na kukosa vibali, Salum alisema boti hizo hazijathibitishwa na Tasac kufanya kazi ya kutoa huduma ya uvushaji, hivyo hakuna uhakika wa usalama wa abiria.
"Boti zao hazijathibitishwa, wanafanya shughuli hizo kinyemela na ni kinyume na utaratibu, wanapaswa kuwa na vibali na Tasac ithibitishe chombo husika," alisema.
Katika kulidhibiti hilo, mkurugenzi huyo alisema askari Polisi wa Kikosi cha wanamaji ndiyo wenye jukumu la kuhakikisha wanafanya doria na kuwakamata wavushaji hao.
"Ni jukumu la Polisi wanamaji kufanya doria na kuwabaini. Tumewahi kusikia taarifa zisizo rasmi kuhusu hilo, lakini mara nyingi wanaofanya hivyo hawana kituo rasmi, tumewahi kwenda lakini huwapati," alisema.
Polisi yafafanua
Akizungumzia hilo, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Wanamaji, Moshi Nisikoro alisema mara nyingi wamekuwa wakiwakamata watu hao.
Kila wanapowakamata katika doria zao, alisema huwapeleka kwa Tasac kwa hatua za kisheria.
Kwa mujibu wa Kamanda huyo, aghalabu watuhumiwa hao hutozwa faini ya Sh500,000 kwa kosa hilo na kwamba ukaguzi unafanyika mara kwa mara.
"Huwa tunafanya doria na tunawakamata wengi, tunawapeleka TASAC na wengi wao wanapiga faini ya Sh500,000 kwa makosa hayo," alisema.
Alipoulizwa kuhusu idadi ya waliokamatwa hadi sasa, alisema ni vigumu kuibainisha kwa kile alichofafanua kua, yupo nje ya ofisi kwa shughuli za mazishi. |
Wizi kwa njia ya mifumo unaendelea kuota mizizi serikalini na sasa umegeukia kwa askari wa usalama b | Wizi kwa njia ya mifumo unaendelea kuota mizizi serikalini na sasa umegeukia kwa askari wa usalama barabarani, huku wanazuoni wakieleza namna unavyofanyika na kupendekeza mbinu za kuudhibiti.
Katika Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, zaidi ya askari 10 kutoka mikoa ya Iringa, Pwani na Kilimanjaro wanadaiwa kuingia matatani kwa wizi huo.
Askari hao, kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi limezipata, wamechepusha fedha zinazopaswa kuingia kwenye mfumo wa Serikali kwa kutengeneza mfumo binafsi kwa ajili ya kupitisha fedha hizo.
Katika wizi huo, inaelezwa askari hao wanatumia mashine za POS (Point of Sale) binafsi na fedha wanazokusanya haziingii serikalini, moja kwa moja zinakwenda kwenye mifuko yao.
Hata hivyo, wataalamu wa mifumo ya kompyuta wanasema wizi huo unafanyika kwa kuingilia mfumo wa malipo wa Serikali, jambo linalowezeshwa na mianya ya usalama katika mfumo huo.
Wizi wa fedha kupitia njia hiyo, uliwahi kushtukiwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika halmashauri kadhaa mkoani Mbeya, akisema zimeunda mfumo nje ya unaotumiwa na Serikali kukusanya fedha.
“Nilikuwa Mbeya hivi karibuni kwenye Nanenane, nikakuta kadhia pale maofisa kabisa wa halmashauri wametengeneza mtandao wao, mbali na ule unaokusanya fedha za Serikali kiuhalisia kuna mwingine wa pembeni na umekusanya fedha nyingi sana.
“Baada ya wao kufanikiwa wakawapa jirani zao, nilikuwa nasubiri ripoti kutoka Tamismi, lakini hajaleta bado na mimi nalijua na naendelea kufuatilia kwa njia zangu, sasa hiyo ripoti ije ikiwa diluted (imechakachuliwa?),” alisema Agosti 17, 2023.
Ukiachana na kilichozungumzwa na Rais Samia, wizi kwa njia hiyo uliibuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Utalii jijini Arusha, Wilbard Chambulo.
Katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda na wadau wa utalii, Chambulo aliibua tuhuma kwa halmashauri ya Jiji la Arusha kumpa fomu ya malipo yenye taarifa tofauti na za kampuni yake.
Sambamba na hilo, mfanyabiashara huyo aliibua tuhuma ya kutozwa ushuru wa Sh24 milioni, lakini risiti aliyopewa iliandikwa amelipa Sh3.6 milioni.
Kuhusu askari wanaotuhumiwa
Vyanzo mbalimbali kutoka katika mikoa hiyo na ndani ya Jeshi la Polisi, vilidokeza kuwa katika mkoa wa Iringa, Askari Trafiki saba wanadaiwa kufukuzwa kazi ndani ya kipindi cha wiki mbili, huku Pwani na Kilimanjaro wakishitakiwa kijeshi.
“Kule Iringa ndio ilikuwa worse (mbaya) kwa sababu mnyororo wa upigaji unadaiwa kumhusisha Afisa mwenye cheo cha juu kidogo. Yeye taratibu zake ziko tofauti kidogo ila naye anachunguzwa,” kilidokeza chanzo kimojawapo.
Kulingana na vyanzo hivyo, Trafiki waliofukuzwa kazi mkoani Iringa wanadaiwa kujihusisha na rushwa na kuchepusha fedha za Serikali zinazotokana na makosa ya usalama barabarani na kujinufaisha nazo binafsi zikiingia katika mifuko yao.
“Tunaambiwa askari wawili walibainika kuwa na ile mashine ya POS (Point of Sale) ya kwao binafsi kwa hiyo wakikusanya fedha haziendi serikalini. Serikali inapaswa ichunguze sana matumizi ya hizi mashine. Kuna kitu hakiko sawa,” kilidai chanzo.
Afisa mmoja wa Jeshi hilo mwenye cheo cha Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP), alilidokeza gazeti hili kuwa baada ya trafiki hao kuhojiwa walimtaja mmoja wa mabosi wao kuwa naye yupo katika mnyororo wa mradi huo wa mapato binafsi.
“Juzi juzi hapa tulikuwa na kikao na Askari ndio tukaambiwa wenzenu huko Iringa wamefukuzwa kazi kwa kucheza na mapato ya Serikali. Huko Pwani nako ni hivyo hivyo kuna askari wako kwenye mashitaka ya kijeshi,” alidai Ofisa huyo.
“Sina hakika sana kama mashitaka yao yamemalizika ama vipi lakini kulikuwa na mashitaka yalikuwa yanaendelea kule Pwani na mchezo ni huo huo tu kama wa Iringa. Inaonekana ni kuna mchezo mchafu kwa baadhi ya Trafiki,” alidai.
Taarifa kutoka mkoani Kilimanjaro, zinadai askari trafiki wanne kutoka wilaya ya Mwanga mkoani humo wamefunguliwa mashitaka ya Kijeshi kwa madai ya kwenda kinyume na mwenendo mwema wa Jeshi hilo unaosisitiza uadilifu.
Taarifa zinadai wiki mbili ama tatu zilizopita, Trafiki hao waliitwa makao makuu ya mkoa kwa Kamanda wa Polisi, Simon Maigwa na kuhojiwa kwa kumiliki kadi binafsi (chip) waliyokuwa wakiiweka kwenye kamera za kubaini mwendo wa gari.
“Ni kweli kuna hilo jambo maana walihojiwa hojiwa sana hapa mkoani tukaona wamevuliwa utrafiki wakawa askari wa kawaida lakini sasa hivi tumeambiwa wamefunguliwa mashitaka ya Kijeshi wanaendelea nayo,” chanzo chetu kilidokeza.
Chanzo hicho kimefafanua kuwa, Trafiki hao kwa miaka miwili, inadaiwa walikuwa wakipiga picha magari yanayovunja sheria kwa kwenda mwendo kasi eneo lisiloruhusiwa, kisha kufanya mazungumzo na madereva na kuchukua fedha.
“Inaonekana wamefanya hili kwa muda mrefu. Wanaingiza Chip yao wanarekodi magari wakishavuta mpunga wanafuta picha na wanaondoa ile chip kama vile magari hayakukamatwa kumbe ni mradi wao,” alidokeza Afisa mmoja.
Ubadhirifu huu unadaiwa kubainika wakati ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2020/2021 ikibaini mashine 89 za POS zinazotumiwa na trafiki kutoza faini hazikuwahi kurekodi muamala wowote.
Katika ripoti hiyo, CAG alibaini kuwapo kwa POS hizo ambazo zilisajiliwa na zilikuwapo hewani katika mfumo wa TMS, hazijawahi kurekodi muamala hata mmoja kwenye mfumo na POS hizo zilisajiliwa kati ya Julai 2019 na Februari 2021.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Msemaji wa jeshi hilo, David Misime alisema bado hajapokea taarifa hizo na kwamba anafuatilia kujua ukweli wake.
“Taarifa za aina hiyo ndiyo nazisikia kutoka kwako, ngoja nifuatilie kuona kama kuna taarifa za namna hiyo,” alijibu.
Hata jana alipotafutwa aeleze iwapo ameshathibitisha, aliendelea kusema majibu aliyoyatoa juzi ndiyo hayo hayo hadi jana.
“Jibu ni lile lile la jana (anaendelea kufuatilia usahihi wa taarifa),” alisema Misime.
Wizi unavyofanyika
Mwanazuoni wa mifumo ya kompyuta wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Fatuma Simba alisema wizi huo unawezekana kwa kuhamisha mfumo.
Alieleza katika malipo ya mtandao kuna mfumo unaowezesha kupeleka fedha kwa mpokeaji aliyelengwa, usipokuwa na ulinzi mahiri, unaweza kuingiliwa na fedha kuhamishiwa njia.
“Kwa vyovyote vile hao watu wameuchezea mfumo, ukiuchezea inakuwezesha kuhamisha kwa kadri unavyotaka,” alieleza mwanazuoni huyo.
Ili kudhibiti hali hiyo kwa mujibu wa Dk Fatuma, kunahitajika ulinzi mahiri wa mfumo husika ili usitoe mwanya wa kuingiliwa na wadukuzi.
“Lazima kila mfumo uwe na ulinzi, hiyo itazuia wenye nia ovu kuuingilia na hatimaye kufanya ubadhirifu. Upo uwezekano wa kufanya hivyo,” alisema.
Licha ya Dk Fatuma kueleza hivyo, mtazamo wa mtaalamu mwingine kutoka chuo hicho, Dk Jimmy Mbelwa ulikuwa tofauti, akifafanua ni vigumu kuingilia mfumo hasa unaohusisha namna ya malipo.
Mtazamo wake huo, unatokana na kile alichoeleza, mfumo wowote huwa na msimamizi ambaye aghalabu huuendesha, nje ya huyo hakuna atakayefanya lolote.
Alikwenda mbali zaidi na kueleza, iwapo itaonekana mfumo hasa wa malipo umeingiliwa, kwa namna yoyote yupo mtu wa ndani kati ya wanaohusika na mfumo amehusika.
“Siamini kwamba mtu anaweza kuingilia mfumo, kwa sababu huwa na usimamizi. Uwezekano wa kuingilia mfumo hasa wa malipo unatokea pale ambapo mtu wa ndani kati ya wasimamizi anapohusika,” alieleza.
Pamoja na mtazamo wake huo, Dk Mbelwa alipendekeza kuangaliwa kwa mianya kwenye mifumo hiyo ili izibwe kudhibiti uwezekano wa kuingiliwa.
Ni mnyororo, ngumu kugundua
Mtaalamu wa ukaguzi wa Hesabu, Edison Leons alisema wizi huo aghalabu unahusisha mnyororo wa watu wakiwemo wenye mamlaka makubwa.
Kinachofanyika, alisema ni kutengenezwa mfumo nje ya ule rasmi kwa ajili ya kupitisha fedha, ambao mara nyingi ni vigumu kuugundia, kwa sababu hufanana.
“Katika mfumo unaotengenezwa, huwa unakuwa na taratibu kama mfumo rasmi, watatumia mshine za POS, utapewa namba ya kumbukumbu ya malipo na risiti ya malipo, lakini fedha zinakwenda kwingineko, sio serikalini,” alisema.
Namna pekee ya kulidhibiti hilo, alisema ni kufuatilia mnyororo wa wahusika wa mfumo, kisha kuwakabili.
Leons ambaye pia ni mkufunzi wa ithibati ya taaluma ya uhasibu (CPA), alieleza nguvu kubwa inahitajika kukabiliana na hilo, kwa kuwa wanaotengeneza huwa ni watu wakubwa. |
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema tayari ameukutanisha Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) | Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema tayari ameukutanisha Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) na Kampuni ya Azam Marine Ltd, kujadili namna bora ya kushirikiana ili kuboresha utoaji huduma ya usafiri wa vivuko katika eneo la Magogoni - Kigamboni.
Kauli hiyo ya Bashungwa inakuja ikiwa ni siku ya pili gazeti la Mwananchi linachapisha mfululizo wa ripoti maalum kuhusu changamoto ya huduma za vivuko katika eneo la Magogoni-Kigamboni.
Msingi wa ripoti hiyo ni uchunguzi uliofanywa kwa takriban miezi mitatu na kuibua changamoto ya ubovu wa vivuko hivyo unaosababishwa na kutofanyiwa matengenezo kwa wakati, kama inavyoelekezwa katika sheria ya Usalama wa Vyombo vya Majini (SOLAS) ya mwaka 1974.
Uchunguzi huo wa Mwananchi umekwenda mbali zaidi na kubainisha namna Temesa inavyopata hasara katika ukodishaji wa vivuko kutoka Azam Marine Ltd, ikilipa kwa kampuni hiyo binafsi Sh300 kwa kila abiria ilhali yenyewe inakusanya Sh200 kwa kila abiria.
Bashungwa ameyasema hayo leo Jumanne Mei 28, 2024 katika mahojiano na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), ambapo amesema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inaimarisha huduma ya usafiri wa vivuko nchini.
"Serikali tumejipanga vizuri kuhakikisha tunaboresha vivuko na tutaweka machaguo kwa abiria ambapo watakuwa na chaguo. Ukitaka kutumia kivuko cha Temesa sawa au ukitaka cha Azam muda mchache kuvuka kwa sababu zile ni ndogo siyo kama kivuko kikubwa ambacho unasubiri kupakia magari na abiria ili muweze kuondoka pamoja," amesisitiza Bashungwa.
Katika mahojiano hayo, waziri huyo amewatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanaotumia usafiri wa vivuko eneo la Kigamboni-Magogoni juu ya taharuki kuhusu huduma inayotolewa na Temesa.
Ameeleza kuwa vivuko vingi vinaendelea na matengenezo, huku vingine vipya vikiendelea na ujenzi chini ya mkandarasi, Songoro Marine katika karakana yake mkoani Mwanza, ili vipelekwe maeneo mbalimbali kutoa huduma kwa wananchi. |
Takriaban wanafunzi 240 wanawake katika Shule ya Sekondari Namanga, wameepukana na safari ya kutoka | Takriaban wanafunzi 240 wanawake katika Shule ya Sekondari Namanga, wameepukana na safari ya kutoka nyumbani kwenda shule, badala yake wataanza kuishi bweni.
Hatua hiyo ni baada ya shule hiyo kukabidhiwa jengo la bweni litakalolaza wanafunzi 240, kutoka kwa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Huduma za Kisheria (LSF).
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi jengo hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa LSF, Lulu Ng'wanakilala amesema dhamira yao ni kuboresha miundombinu ya shule.
Lengo lingine la msaada huo walioutoa kwa kushirikiana na North-South Cooperation kutoka Luxemburg, unalenga kuwawezesha wanafunzi, hasa wasichana, kupata haki yao ya elimu bora.
"Mradi unashughulika na mila potofu zinazowakandamiza wanawake na wasichana na kupambana na ukatili wa kijinsia katika jamii.
“Aidha, mradi huu unalenga kuwawezesha wasichana kutimiza ndoto, kuhakikisha usalama wao dhidi ya ukatili wa kijinsia wakiwa shuleni na kukuza uendelevu wa mazingira kwa kupanda miti," amesema.
Ameeleza bweni hilo litawapa wanafunzi hao mazingira mazuri ya kujifunza.
Meneja Mkuu wa North-South Cooperation, Roberto Marta, amesema ni miaka miwili sasa tangu washirikiane na LSF na bweni hilo ni moja ya matunda.
“Tunafurahi kuona wasichana wa Kimasai sasa watakuwa na mazingira mazuri ya kusomea. Serikali ya Luxemburg inajivunia kuunga mkono miradi inayoboresha maisha ya kijamii na kiuchumi,” amesema.
Mkuu wa Wilaya ya Longido, Marko Ng'umbi amesema jengo hilo linaibua matumaini na fursa kwa wanafunzi kujisomea katika mazingira bora na rahisi.
"Juhudi hii bila shaka itakuwa na alama ya kudumu katika maisha ya vijana wetu, ikiwapa mazingira wanayohitaji ili kufaulu katika masomo yao na kufikia ndoto zao,” amesema. |
Magonjwa kama homa ya mapafu na mengine yanayohusiana na baridi, yanatarajiwa kuwakabili wananchi ka | Magonjwa kama homa ya mapafu na mengine yanayohusiana na baridi, yanatarajiwa kuwakabili wananchi katika kipindi cha kuanzia Juni hadi Agosti mwaka huu.
Uwezekano wa kutokea kwa magonjwa hayo, unatokana na matarajio ya kuanza kwa msimu wa kipupwe (JJA), utakaosababisha hali ya baridi ya wastani na joto kiasi.
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), katika kipindi hicho kunatarajiwa pia kuwepo na vumbi linalosababishwa na upepo katika baadhi ya maeneo na hivyo kuibua magonjwa ya macho.
Hizo ni baadhi ya tahadhari zilizotolewa leo, Jumatatu Mei 27, 2024 na TMA ikitahadharisha matokeo ya msimu wa kipupwe utakaoanza Juni mwaka huu.
Sambamba na tahadhari hizo, nyingine zilizotolewa na mamlaka hiyo ni uwezekano wa kutokea magonjwa ya mifugo na macho kutokana na vumbi.
“Tunatoa tahadhari za kiafya zichukuliwe ili kulinda jamii dhidi ya magonjwa yanayoweza kusababishwa na baridi na vumbi hilo,” imeeleza taarifa hiyo.
Kutokana na hali ya ukavu inayotarajiwa katika maeneo mengi kwa kipindi hicho, TMA inapendekeza maji na malisho yatumike kwa uangalifu ili kupunguza athari inayotarajiwa kujitokeza.
“Wakulima wanashauriwa kulima mbogamboga na mazao ya mizizi kama vile viazi katika maeneo unyevu na maeneo yanayotarajiwa kupata vipindi vya mvua katika kipindi huo,” amesema.
Hali itakavyokuwa
Katika kipindi hicho, Mikoa ya Kusini mwa Morogoro, Mbeya, Songwe, Iringa na Njombe inatarajiwa kupigwa baridi ya wastani hadi kali.
"Vipindi vya baridi zaidi vinatarajiwa kujitokeza kati ya Julai mwaka huu ambapo joto la chini linatarajiwa kuwa kati ya nyuzi joto 7 na nyuzi joto 15 na katika maeneo yenye miinuko kiwango hicho kinatarajiwa kuwa chini ya nyuzi joto 7," imesema TMA.
Kwa Mikoa ya Mwanza, Mara, Geita, Kagera, Shinyanga na Simiyu, taarifa hiyo inaeleza hali ya baridi ya wastani na joto kiasi inatarajiwa na kiwango cha joto la chini kinatarajiwa kuwa kati ya nyuzi joto 15 na 20.
Kwa upande wa Dar es Salaam, Pwani, Tanga, maeneo ya kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro na visiwa vya Unguja na Pemba, hali ya baridi ya wastani na joto kiasi inatarajiwa na kiwango cha joto la chini kitakuwa kati ya nyuzi joto 23 na 26.
Lakini maeneo ya mwambao wa Pwani na visiwani hali itakuwa kati ya nyuzi joto 17 na 23, huku maeneo yenye miinuko yanatarajiwa kuwa na kiwango cha nyuzi joto chini ya 17.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kilimanjaro, Arusha na Manyara inatarajiwa kukumbwa na hali ya baridi ya wastani hadi joto kiasi, huku maeneo yenye miinuko yanatarajiwa kuwa na joto la chini kati ya nyuzi joto 15 na 20.
Mikoa mingine itakayokabiliwa na baridi la wastani na joto kiasi ni Tabora, Rukwa, Katavi na Kigoma na kwamba joto la chini kwa mujibu wa TMA, litakuwa kati ya nyuzi joto 15 na 20.
Kusini mwa Mkoa wa Katavi yanatarajiwa kuwa na baridi ya wastani hadi baridi kali chini ya nyuzi joto 15.
Kanda ya kati mikoa ya Singida na Dodoma hali ya baridi ya wastani hadi joto kiasi inatarajiwa katika maeneo mengi ambapo joto la chini linatarajiwa kuwa kati ya nyuzi joto 11 na 17.
TMA imesema ukanda wa Pwani ya Kusini inayohusisha Mikoa ya Mtwara na Lindi hali ya baridi ya wastani hadi joto kiasi inatarajiwa katika maeneo mengi na itafikia nyuzi joto 17 na 22
Mkoa wa Ruvuma hali ya baridi ya wastani hadi baridi kali inatarajiwa katika maeneo mengi ambapo joto la chini linatarajiwa kuwa kati ya nyuzi joto 10 na 18.
Kwa upande wa mwenendo wa upepo TMA imesema msimu wa Kipupwe hutatawaliwa na upepo wa kusi unaotarajiwa kuwa wa wastani hadi upepo mkali utakaovuma kutoka kusini mashariki na vipindi vichache vya upepo wa kusi katika ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na maeneo ya nchi kavu.
Pia TMA imesema kipindi cha msimu wa Kipupwe kinatawaliwa na hali ya ukavu katika maeneo mengi ya nchi hata hivyo vipindi vichache vya mvua vinatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kagera, Geita, Simiyu na Mara, kaskazini mwa Kigoma, Arusha na Kilimanjaro na Dar es Salaam, Tanga, Morogoro, Mtwara, Lindi, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba. |
Mashaka ya kukamilika kwa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) yanaendelea kupata mashiko, baada ya kuendel | Mashaka ya kukamilika kwa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) yanaendelea kupata mashiko, baada ya kuendelea kushuhudiwa ahadi zisizotimia katika za kukamilishwa utekelezwaji wa vipande mbalimbali.
Sambamba na ahadi zisizotimia, kumeshuhudiwa makundi ya wafanyakazi katika kambi mbalimbali wakiondolewa kambini na mkandarasi kwa kile kinachodaiwa, Serikali haina fedha ya kumlipa kuendelea na kazi.
Ukurasa wa ahadi zilizo za kweli, ulifunguliwa katika utekelezwaji wa kipande cha kwanza cha mradi wa SGR kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro, kilichotakiwa kukamilika kwa miezi 30, lakini ilishindikana na kuongezewa miezi 18.
Ukiachana na ahadi hiyo na nyingine nyingi, kipande cha tano cha Isaka-Mwanza kilichopaswa kukamilika Mei 14, mwaka huu nacho kimevuka matakwa ya mkataba.
Kamati ilivyoonyesha mashaka
Mashaka ya kukamilika kwa ahadi ya utekelezwaji wa kipande cha Isaka-Mwanza, yalionyeshwa hata na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundimbonu.
Katika hotuba yake bungeni jijini Dodoma Aprili mwaka huu, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Selemani Kakoso alishuku iwapo kipande hicho cha mradi wa SGR kitakamilika kwa wakati.
Msingi wa mashaka yake ni kukaribia kwa siku inayopaswa kuwa mwisho wa mradi, ambayo ni Mei 14, mwaka huu lakini hatua za utekelezaji zikiwa katika asilimia 54.01.
Mbali na mashaka hayo, katika hotuba yake hiyo Kakoso alisema Serikali imeshamlipa mkandarasi Sh1.343 trilioni, sawa na asilimia 40.53 ya gharama ya mradi.
“Kamati ina mashaka kuhusu muda uliobaki kukamilsha Mradi husika kufikia Mei, 2024 ukilinganisha na asilimia iliyobaki ya ujenzi.
“Serikali ilitaarifu Kamati kwamba, wana matumaini kuwa Mkandarasi atakamilisha ujenzi kwa sababu kazi iliyobaki sio kubwa ukilinganisha na kazi iliyofanyika tayari,” alisema.
Hata hivyo, tayari tarehe iliyopangwa kwa ajili ya mradi huo kukamilika imeshapita na bado kazi hazijaisha.
Kwa muibu wa Kakoso katika hotuba yake hiyo, kamati imebaini kuwepo kwa malalamiko ya wananchi kutokana na kutolipwa fidia baada ya maeneo yao kutwaliwa kupisha mradi.
Alipendekeza Serikali ifanikishe malipo ya wananchi hao kwa mujibu wa sheria.
Fedha tatizo
Danadana na kuchelewa kwa mradi huo pamoja na mingine ya SGR, kunahusishwa na changamoto za kifedha ambazo Serikali inadai kushindwa kumlipa mkandarasi CCECC kutoka Jamhuri ya Watu wa China, akamilishe kazi hiyo.
Hilo, linathibitishwa na baadhi ya wafanyakazi katika kambi mbalimbali za mradi huo, wanaolalamikia kuondolewa kazini kwa kile walichoambiwa na mkandarasi, Serikali haina fedha za kulipa ili mradi uendelee.
Mmoja wa wanaofanya kazi katika mradi huo kipande cha Isaka-Mwanza (jina lake limehifadhiwa), alisema katika kambi yao walianza wakiwa wafanyakazi zaidi ya 400 lakini waliosalia sasa ni 50.
Katika kambi hiyo ya Luvumbo, mfanyakazi huyo alisema upunguzaji wa wafanyakazi ulianza Aprili 20, mwaka huu walipopunguzwa watu zaidi ya 100.
Kwa mujibu wa mfanyakazi huyo, upunguzaji uliendelea hadi kumfikia yeye na sasa wamesalia wafanyakazi 50 katika kambi hiyo.
“Sisi tulipunguzwa Ijumaa (Mei 24) waliobaki ni kama wafanyakazi 50 hivi na hata magari yameanza kuondolewa kuna dalili kwamba mradi umekwama,” alieleza.
Sababu ya kupunguzwa kwao ni kile alichoeleza, wamearifiwa na Idara ya Rasilimali watu kuwa, kuna changamoto za kifedha zinazofanya washindwe kulipwa.
“HR alipita na kutwambia kwamba Serikali haina fedha ya kumlipa mkandarasi aendelee na kazi, kwa hiyo tumetakiwa kwenda nyumbani kwa mwezi mmoja kisha wameahidi wataturudisha,” alieleza.
Kuhusu malipo ya kusitishiwa mikataba, alieleza kwa waliokuwa na mikataba ya matazamio yaani miezi mitatu, mkandarasi ameahidi kuwalipa siku nne za ziada.
Lakini kwa wale waliokuwa wameshafanyakazi kwa zaidi ya miezi sita, alisema wanalipwa hela ya likizo ya mwaka mmoja kwa hesabu ya Sh16,600 kila siku.
Alieleza hatua hiyo ni pigo kwake, kwani imetokea ghafla, ingawa wengine wapo kambini yeye ameamua kuondoka kwa kukosa fedha za kujigharimia.
Katika kutafuta ukweli wa hayo, Mwananchi iliwasiliana kwa njia ya simu na Meneja Rasilimali watu wa kampuni ya Yepi Merkez aliyegoma kutaja jina lake, alielekeza atafutwe msemaji, kwani si mamlaka yake kuzungumzia kampuni.
"Siwezi kuzungumzia hilo mtafute mtu wa mawasiliano au Meneja mradi,"amesema.
Hata alipotafutwa msemaji huyo, simu yake iliita bila majibu.
Hata hivyo Meneja wa mradi huo alipotafutwa naye alidai tayari alishaondoka kabla ya barua kusambazwa kwa wafanyakazi wengine.
Mkutopora-Tabora nao hali tete
Wengine waliokumbwa na kadhia hiyo ni wale wanaofanya kazi katika kipande cha Makutopora hadi Tabora chenye urefu wa Kilomita 368.
Kwa mujibu wa mmoja wa wafanyakazi hao, waliarifiwa kuwa hakutakuwa na kazi katika eneo hilo hadi pale watakapopigiwa simu na kwamba tangu Septemba mwaka jana zaidi ya watu 1,000 wamepunguzwa.
Kipande hicho cha SGR kinachotekelezwa na mkandarasi Yapi Merkezi, mfanyakazi huyo anadai sababu ya kupunguzwa kwao ni Serikali kukosa fedha ya kumlipa mkandarasi.
Tangazo la Yapi Merkezi lililotolewa juzi liliwaelekeza wafanyakazi wote kuwa, “kuanzia Mei 23/2024 hakutakuwa nα kazi hadi mtakapoarifiwa na idara ya rasilimali watu na wakuu wa idara husika kurudi kazini. Tafadhali hakikisha simu yako inapatikana muda wote," iliandikwa kwenye tangazo hilo.
Mfanyakazi huyo alisisitiza mkandarasi amewaarifu kuwa hana fedha kwa sababu muajiri wake (Serikali), imeishiwa.
"Yapi Merkezi wametuambia hawana fedha Serikali imeishiwa hela ya kuendelea na mradi, hali si nzuri miradi mingi nimewasiliana na wenzangu inasuasua hivyo watu wengi wamerudishwa nyumbani, mimi nimesimamishwa kuanzia Februari," alisema.
Mfanyakazi mwingine katika mradi huo, alisema ameona tangazo hilo katika kipindi ambacho tayari alishaondolewa kazini tangu Februari mwaka huu.
"Tunaomba Serikali imlipe Yapi Merkezi hatuna kazi za kufanya mimi nipo nyumbani tu, nimeambiwa nitapigiwa simu lakini sijui nini kitatokea huenda ndio mwisho wa ajira zetu," alisema.
Kipande hicho cha Makutupora-Tabora kinagharimu Sh4.606 trilioni na matarajio ya kukamilika kwake ni ndani ya miezi 42 kuanzia Aprili mwaka 2022.
Serikali yaahidi kuendelea na kazi
Pamoja na kuwepo kwa uhalisia huo, katika hotuba yake ya Mei 6, mwaka huu Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisema Serikali inaendelea na ujenzi wa mradi huo kwa awamu zote mbili zenye jumla ya mtandao wa kilomita 2,809.
Sambamba na awamu hizo, waziri huyo alisema Serikali itaendelea na ujenzi wa reli hiyo kwa maeneo mengine ya Ushoroba wa Kusini na Kaskazini kwa kadri ya upatikanaji wa rasilimali fedha.
Katika mazungumzo yake hayo, Profesa Mbarawa alisema utafutaji wa fedha kutoka kwa wadau unaendelea, wakiwemo wawekezaji kwa ubia baina ya sekta ya umma na binafsi (PPP).
Ushirikiano huo, kwa mujibu wa Mbarawa unalenga kufanikisha ujenzi wa reli hiyo kwa maeneo yaliyobaki yanayojumuisha kutoka Kaliua – Mpanda – Karema (kilomita 321), Isaka – Rusumo – Rwanda (kilomita 371), Mtwara – Mbambabay na matawi ya Liganga na Mchuchuma (kilomita 1,000).
Vipande vingine ni Tanga – Arusha – Musoma (kilomita 1,028), Reli ya Jiji la Dar es Salaam (kilomita 166) na Reli ya Jiji la Dodoma (kilomita 107).
Alieleza mahitaji makubwa ya fedha za utekelezaji wa miradi ya uchukuzi kuhitaji fedha nyingi (capital intensive) katika utekelezaji wake. Mathalan,Mradi wa SGR utagharimu takriban Shilingi trilioni 23 hadi kukamilika kwake.
Ukiachana na maelezo yake ya Mei 6, mwaka huu, Mwananchi jana, lilimtafuta tena Profesa Mbarawa azungumzie madai yote, simu yake iliita bila majibu.
Hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maandishi na kwa njia ya WhatsApp ilionyesha umefiwa, lakini haukujibiwa.
Pamoja naye, alitafutwa pia Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Godius Kahyarara, alipokea na kudai yu kikaoni na kwamba angepiga simu baada ya kutoka.
Hadi habari hii inamaliza kuchapwa mtendaji mkuu huyo wa wizara hiyo hakumtafuta tena mwandishi na hata alipotafutwa simu yake iliita bila kupokelewa. |
Mifumo ya uendeshaji iliyojikita katika utoaji huduma badala ya kufanya biashara, ni moja ya mambo y | Mifumo ya uendeshaji iliyojikita katika utoaji huduma badala ya kufanya biashara, ni moja ya mambo yanayotajwa kuuweka rehani uhai wa Wakala wa Huduma na Umeme Tanzania (Temesa), Mwananchi imebaini.
Mifumo hiyo kwa mujibu wa uchunguzi wa takriban miezi mitatu uliofanywa na gazeti hili, inaisababisha Temesa kufanya kazi katika mazingira magumu na hata kukabiliwa na lindi la madeni.
Kupitia uchunguzi huo, Mwananchi imebaini wakala huo licha ya kutekeleza hukumu la matengenezo ya magari ya taasisi za Serikali, haijalipwa mabilioni ya fedha zake.
Hali hiyo, imechagiza wakala huo kuingia madeni ya zaidi ya Sh35 bilioni kutoka kwa wazabuni wake ambao ni sekta binafsi wanaowasambazia vipuli kwa ajili ya matengenezo ya magari hayo.
Mfumo wa utendaji
Katika mazungumzo ya Mwananchi na mmoja wa maofisa waandamizi wa Temesa (jina lake limehifadhiwa) anaeleza mfumo wa utendaji wa wakala huo upo katika misingi ya utoaji huduma.
Hilo linatokana na kile anachoendeleza, sheria ya kunzishwa kwa wakala huo ya mwaka 2005, inautaja wakala huo kuwa taasisi ya Serikali yenye lengo la kuhudumia na sio kufanya biashara.
Anasema mifumo inataka itoe huduma ilhali uhalisia wa shughuli za Temesa, zina sura ya kibiashara.
“Temesa inajihusisha na matengenezo ya magari ya taasisi na wakala za Serikali, pia inahusika na uendeshaji wa vivuko, hizi shughuli zote tunakusanya mapato na kimsingi ni biashara, unapotaka tutoe huduma hatutapata kinachotarajiwa,” anasema.
Matengenezo magari ni janga
Chanzo kingine cha kuaminika ndani ya Temesa, kimeiambia Mwananchi kuwa, wakala huo upo mahututi kutokana na kukabiliwa na madeni.
Anasema kwa sababu wakala huo hauna mtaji, unalazimika kusimama katikati ya wazabuni wenye vipuli ambao ni sekta binafsi na Taasisi za Serikali zenye magari.
Kwa sababu hiyo, anasema wanakopa vipuli kutoka kwa wazabuni ambao ni sekta binafsi kwa ajili ya kutengeneza magari ya taasisi za Serikali zikiwemo halmashauri.
“Tunakopa kwa hawa wazabuni, tunatengeneza magari ili wakitulipa (taasisi za Serikali) nasi tunawalipa wazabuni wetu,” anasema.
Lakini, kazi hiyo ya matengenezo ya magari, anasema imekuwa janga kwa Temesa kwani wateja wake ambao ni taasisi za Serikali hazilipi gharama za matengenezo.
“Na hii sio kwa Temesa yaani ni suala la mtazamo wa taasisi nyingi, zinapoona huduma inatolewa na wakala au taasisi nyingine ya Serikali huwa hazilipi,” anaeleza.
Kutokana na mazingira hayo, anaeleza wakala huo umebaki kudaiwa na wazabuni wake wanaoisambazia vipuli kwa kuwa fedha za kuwalipa zipo kwa wateja.
Mwananchi linayo taarifa ya mwisho ya madeni hayo ambayo Temesa iliyowasilisha Hazina, ikieleza wakala huo unadai takriban Sh40 bilioni kwa taasisi hizo za Serikali.
Kulingana na taarifa hiyo ya mwanzoni mwa mwaka huu, pamoja na Temesa kudai kiasi hicho cha fedha na yenyewe inadaiwa zaidi ya Sh35 bilioni na wazabuni wake.
Madeni inayodaiwa Temesa yametokana na kushindwa kuwalipa wazabuni hao, baada ya wakala huo kukopa vipuli ikitarajia kulipa itakapolipwa gharama za matengenezo.
Mbali na chanzo hicho, Ofisa mwingine ndani ya Temesa, anasema katika kila mwaka kwa wastani kuna asilimia 60 hadi 70 ya madeni ya kudai ha kudaiwa yanayovuka mwaka mwingine wa fedha.
“Kwa hiyo ni kweli tunadaiwa kwa sababu nasi hatulipwi,” anasema ofisa huyo.
Hawana nguvu ya kudai
Ofisa huyo, anasisitiza ugumu wa kulipwa unatokana na wakala huo kukosa nguvu ya kisheria katika kukusanya madeni yake.
“Unamdai mtu lakini huna kitu chake chochote ulichoshika kama dhamana, ambacho unasema asipolipa nitauza hiki na hata hivyo haruhusiwi kukama gari hata kama unalidai.
“Benki zingekuwa zinakopesha na hazichukui dhamana ingekuwa hatari na hivyo ndivyo tunavyofanya kazi, unamkopesha mtu na huna kitu chochote chake kwa ajili ya kushinikizia malipo yako,” anasema.
Walivyoshindwana na Toyota
Kama unakumbuka mwaka mmoja uliopita kulikuwa na shinikizo la Temesa kushirikiana na Kampuni ya Toyota na pengine usijue yalipoishia.
Mifumo ya utendaji wa Temesa ndiyo yaliyokwaza ushirikiano huo, baada ya Toyota kuweka masharti magumu ambayo pengine yasingekuwa na tija kwa wakala huo.
Mazingira kama hayo yalisababisha hata ushirikiano kati ya wakala huo na kampuni ya Toyota ushindikane.
Kwa mujibu wa ofisa wa Temesa, katika ushirikiano huo walianza kwa kukaa vikao, timu za uratibu wa shughuli ziliundwa na ulifikia wakati wa kujua masharti gani Toyota inatoa ili kufanya kazi na wakala huo.
“Walileta orodha hiyo balaa… kwanza wakataka kwenye bajeti ya matengenezo ya magari inayotolewa na Serikali asilimia 50 iingizwe kwao,” anaeema.
Sharti lingine, anasema Toyota ilitaka anapopatikana mteja, fedha za vipuli zilipwe kwao, huku ufundi ndiyo ilipwe Temesa.
Iwapo hilo lingetokea, anasema Toyota ingekuwa na nguvu ya kukamata magari ambayo hayatalipia huduma na Temesa ingekufa kwa kukosa fedha za kujiendesha.
“Temesa haitaweza kujiendesha kwa mapato ya ufundi pekee ni madogo mno,” anasema.
Anasisitiza kushindikana kwa hayo, kumetokana na ukweli kwamba, bado Serikali haijajua inataka kutoa huduma au biashara kwa Temesa.
Akizungumzia hilo, Mtendaji Mkuu wa Temesa, Lazaro Kilahala anasema mipango ya mabadiliko ya utendaji wa wakala huo inaendelea.
Anataja mipango hiyo pamoja na mambo mengine, inahusisha mageuzi ya utendaji ili kuhakikisha wakala huo unazalisha faida katika hughuli zake.
Hata hivyo, Kilahala alikiri wakala huo kuwa na madeni kutoka kwa wazabuni na kwamba yanalipwa kwa kadri fedha zinavyopatikana.
“Wadeni wote wanaolipwa kwa mujibu wa taratibu, msisitizo ni kuhakikisha wakala unakuwa na ufanisi ndiyo maana tunatarajia kufanya mageuzi ya utendaji wa wakala,” anasema.
Taasisi zenyewe zinasemaje
Mkuu wa Idara ya Fedha wa moja ya Halmashauri jijini Dar es Salaam (jina lake limehifadhiwa) anasema bajeti za OC za halmashauri mbalimbali nchini hazihusishi matengenezo ya magari.
Anasema kwa kuwa hakuna bajeti hizo kutoka Serikali kuu, Halmashauri zinazalimika kukopa matengenezo na zinashindwa kulipwa kwa sababu, hakuna pa kupata.
“Si umeona magari mengi ya Serikali kwenye Halmashauri yakiharibika kidogo tu, yanaachwa yanaoza, sababu ya yote haya ni kukosekana kwa bajeti ya matengenezo ya magari, tunabeba hivyo hivyo,” anasema.
Namna ya kutatua
Ili kutatua changamoto hizo, Mwanazuoni wa biashara za Kimataifa, Profesa Francis Matambalya anasema kuna umuhimu wa kubadilishwa kwa sheria ya kuanzishwa kwa Temesa ili wakala huo, ujiendeshe kibiashara.
Katika mabadiliko hayo ya sheria, anapendekeza suala la uendeshaji wa vivuko liondolewe chini ya wakala huo na utafutwe utaratibu mwingine.
“Pia, iwe taasisi tendaji isiwe wakala kwa sababu inakuwa na watu wengi wenye maamuzi, hata unapofukuza watumishi iwe kwa sababu za kitendaji na sio maelekezo ya mwenye maamuzi,” anasema.
Pendekezo kama hilo, limetokewa na mmoja wa maofisa waandamizi wa Temesa, alipozungumza na Mwananchi.
Kwa mujibu wa Ofisa huyo, uendeshaji wa vivuko ni moja ya majukumu yanayoibebesha mzigo Temesa, kuna umubimu wa kutenganisha.
“Ianzishwe kampuni kwa ajili ya kuendesha vivuko, wakati shughuli za utengenezaji wa magari ndiyo ziachwe kwa Temesa, kuipunguzia mzigo,” anasema. |
Licha ya dhamira ya Serikali ya kushirikiana na sekta binafsi katika utoaji wa huduma ya vivuko Kiga | Licha ya dhamira ya Serikali ya kushirikiana na sekta binafsi katika utoaji wa huduma ya vivuko Kigamboni na Magogoni, huenda mpango huo ukabaki kuwa ndoto isiyotimia.
Kutotimia kwake, kunatokana na uhalisia wa mazingira yaliyowekwa na Serikali ya utoaji huduma katika eneo hilo, ambayo si rafiki kwa sekta binafsi.
Nia ya Serikali kushirikiana na sekta binafsi katika utoaji huduma ya vivuko katika eneo hilo, iliwahi kuwekwa wazi na Rais Samia Suluhu Hassan Novemba 11, 2022.
Katika hotuba yake alipokuwa akizindua mradi wa maji, wilayani Kigamboni, Rais Samia alionyesha nia ya kushirikiana na sekta binafsi, akilenga kuboresha huduma za vivuko.
“Tunatambua kuna kivuko kinafanyiwa matengenezo, kuna kivuko kipya kinajengwa. Tutaingia mkataba na sekta binafsi ili kuendesha huduma za vivuko,” alisema.
Mzizi wa kauli hiyo ya Rais Samia, ni hoja ya Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile aliyelalamikia huduma mbovu za vivuko katika eneo hilo.
Msisitizo wa hoja yake hiyo, Dk Ndugulile ulikuwa ni kuiomba Serikali iiruhusu sekta binafsi iwekeze katika utoaji wa huduma za vivuko ili kuongeza ufanisi.
“Tunaomba kama inawezekana kivuko hicho kikabidhiwe kwa sekta binafsi,” alisema Mbunge huyo.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwepo mazingira yasiyoshawishi kibiashara kwa sekta binafsi kuwekeza katika uendeshaji wa vivuko kwa kushirikiana na Serikali.
Mazingira ya biashara
Nguvu ya kisiasa, inatajwa kuchagiza ugumu wa sekta binafsi kuwekeza katika utoaji wa huduma za vivuko katika eneo la Kigamboni na Magogoni.
Hilo linathibitishwa na mmoja wa maofisa wa Serikali aliyezungumza na Mwananchi kwa sharti la kutotajwa jina, akisema dhamira ipo lakini hakuna mazingira wezeshi.
Kwa mujibu wa ofisa huyo ndani ya Wakala wa Huduma na Umeme Tanzania (Temesa), sekta binafsi inataka uhuru wa kupanga mambo yake ili izalishe faida.
Lakini upande wa Serikali, anasema bado kuna mtazamo wa utoaji huduma na si kibiashara, hivyo inang’ang’ana kupanga kiwango cha nauli kwa mwekezaji yeyote atakayetaka kuwekeza katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa ofisa huyo, Serikali imetoa sharti kwa mwekezaji yeyote atakayewekeza katika eneo hilo, asitoze nauli zaidi ya Sh300.
“Kiwango hicho cha nauli hakiwezi kurudisha gharama za uwekezaji, itakuwa hasara kwa mwekezaji, ndiyo maana wawekezaji wanaogopa,” anasema.
Anasema kuna haja ya Serikali kuona umuhimu wa kumwachia mwekezaji apange bei kulingana na gharama za uendeshaji, ili naye apate faida.
“Angalau wangeruhusiwa kutoza Sh500 ingekuwa sawa, lakini kwa hizi nauli za Sh200 hakuna mwekezaji aliye tayari,” anasema.
Hata hivyo, Mwananchi linazo taarifa za Temesa kuzifuata kampuni kadhaa ikiwemo Azam Marine Ltd kwa ajili ya kuomba ushirikiano nayo katika utoaji huduma, lakini kampuni hiyo haijaonyesha nia.
“Wamefuatwa mara kadhaa na wameahidi kuandaa pendekezo, lakini imeshapita miaka miwili tangu waahidi hivyo kila wakiulizwa wanajibu hawajakamilisha,” anasema mmoja wa maofisa wa Temesa.
Sambamba na kauli ya Ofisa huyo wa Temesa, Mwananchi ilimtafuta mmoja wa viongozi wa moja ya kampuni binafsi inayojishughulisha na utoaji wa huduma za vivuko, anasema ni vigumu kuwekeza katika eneo hilo.
Anaeleza ingewezekana kuwekeza iwapo, angepewa fursa ya kupanga nauli kwa kila abiria kupitia tathmini ya gharama za uendeshaji na sio kupangiwa na Serikali.
“Nauli za mabasi zinaongezeka kila siku kwa sababu ya kuongezeka kwa bei ya mafuta, huwezi kunipangia bei ya nauli ya kivuko wakati mimi najua nagharamikaje na uendeshaji.
“Kingine sisi ni sekta binafsi hatutoi huduma kaka Serikali, mimi sina ruzuku nitakachopata kama faida ndicho nitakitumia kugharimia uendeshaji,” anasema.
Anasisitiza umuhimu wa mabadiliko ya sheria ya kuanzishwa kwa Temesa na kiundwe chombo kitakachodhibiri usafiri wa majini kama ilivyo Latra ardhini.
Anaeleza chombo hicho ndicho kiwe msimamizi wa wadau wote wa usafirishaji majini na hata nauli itahakikisha zinatozwa kwa kuzingatia mazingira yaliyopo.
Ukiachana na mwekezaji huyo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Songoro Marine Ltd, Major Songoro anasema bado hana fikra ya kufanya uwekezaji huo.
Ingawa hakuweka wazi sababu za kutokuwa na fikra hizo, Songoro anasema haoni kama atafaidika, akisisitiza watoa huduma wengine wa vivuko wanaweza kwenda kuwekeza.
“Sisi hilo halipo kwenye mipango yetu na hatuna nia hiyo kabisa, labda kama kuna watoa huduma binafsi wa vivuko waende kuwekeza,” anasema.
Imebainika kuwa, wawekezaji hao waliowahi kufuatwa mara kadhaa na Serikali kwa ajili ya kutakiwa kuwekeza, wanajizungusha kwa makusudi kwa kuwa hawaoni faida katika uwekezaji huo.
Wanazuoni
Mhadhiri wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Juma Kapaya anasema kuna umuhimu wa Serikali kuita wawekezaji wote kutoka sekta binafsi kwa ajili ya mazungumzo nao.
Mazungumzo hayo, anasema yalenge kujadili gharama za utoaji huduma katika eneo hilo, kisha wasikilizwe wawekezaji wangehitaji kutoa kiasi gani cha nauli ili kumudu uendeshaji.
“Kwa sababu mwekezaji anaangalia gharama, Serikali yenyewe ni kama mzazi anahudumia, lakini sekta binafsi inafanya biashara, kwa hiyo wakae meza moja wajadili hilo,” anasema.
Kwa mtazamo wa Kapuya, kuwepo kwa sekta binafsi katika eneo hilo, kutaboresha huduma za vivuko na kuwanufaisha wananchi.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, alitaka atafutwe Mtendaji Mkuu wa Temesa, Lazaro Kilahala kwa ufafanuzi zaidi.
Katika kauli yake Kilahala anasema mpango wa kushirikiana na sekta binafsi upo na kwamba tayari mazungumzo na wawekezaji kadhaa akiwemo Azam Marine Ltd yanaendelea.
Alipoulizwa kuhusu Serikali kulazimisha nauli ya kutoza, anasema kwa kuwa majadiliano na wawekezaji yanaendelea, utafika wakati kila kikwazo kitatatuliwa. |
Kama umewahi kuhisi maumivu ya kutwishwa mzigo wenye uzito zaidi ya nguvu zako halisi, basi hali hiy | Kama umewahi kuhisi maumivu ya kutwishwa mzigo wenye uzito zaidi ya nguvu zako halisi, basi hali hiyo inaukabili Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), katika jukumu la uendeshaji wa vivuko nchini.
Temesa inatekeleza jukumu hilo kwa mujibu wa sheria ya kuanzishwa kwake ya mwaka 2005, inayotaka pamoja na majukumu mengine ya msingi, wakala huo uwajibike na uendeshaji wa uhakika na usalama wa vivuko nchini.
Jukumu hilo la kisheria badala ya kuwa fursa ya mapato kutokana na makusanyo ya vivuko, limegeuka shubiri na mzigo mzito kwa Temesa na uchunguzi uliofanywa na Gazeti la Mwananchi kwa takriban miezi mitatu umelibaini hilo.
Kilichochagiza uchunguzi huo, ni malalamiko ya wananchi wanaotumia huduma za vivuko hivyo, ambao mara kadhaa wamelalamika kutoridhishwa nazo.
Msingi wa malalamiko yao ni kuchelewa kwa huduma wanapofika katika eneo la kuvuka, kuharibika mara kwa mara kwa vivuko na hata uchache wake, kama inavyoelezwa na Salma Ally mkazi wa Kigamboni.
Wananchi wanavyolalamika
Salma anayefanya biashara ya samaki Kibugumo, katika Wilaya ya Kigamboni, anasema inamchukua saa moja na zaidi kusubiri kuvuka Kigamboni-Magogoni.
Hiyo ni tofauti na matarajio yake, anayosema ni kutumia dakika 20 hadi 30 kuvuka katika eneo hilo kwa ajili ya kwenda lilipo soko la samaki Ferry.
“Ukitaka kufuata samaki ujue kabisa ukishafika hapa kwenye jengo la abiria utapoteza saa au zaidi kusubiri kivuko,” anasema Salma.
Anachokisema Salma kinashabihiana na Abudi Abedi anayefanya biashara hiyo ya samaki, anayesema analazimika kuamka asubuhi zaidi kuwahi sokoni.
“Natoka saa 10 alfajiri nyumbani Cheka, Kigamboni lakini nafika sokoni saa 12 na wakati mwingine saa 1 asubuhi, panaponichelewesha ni eneo la kuvuka,” anasema.
Hali duni ya vivuko imewahi kuzua hofu kwa Mauwa Mussa anayeishi Kigamboni, baada ya kivuko kuzima katikati ya maji akiwa ndani yake.
“Sitaki kukumbuka ilivyokuwa, kila mmoja alikuwa anafanya sala anayoiamini, nilikata tamaa kwamba nisingeweza kupona kwa sababu hata kutumia maboya siwezi,” anasema.
Mauwa anasimulia hadi kivuko kinavutwa na watu kushuka hakuwa na fahamu na hata mizigo aliyokuwa nayo haikuwepo.
“Waliniibia mizigo yote baada ya kupoteza fahamu, nikipata hasara, wasiwasi na hadi sasa napenda kivuko roho ikiwa mkononi, siviamini hivi,” anasema Mauwa.
Yaliyomkuta Mauwa ndiyo yaliyosababisha Asajile Michael akome kutumia vivuko kuvuka na gari lake, badala yake anazunguka kupitia Daraja la Mwalimu Julius Nyerere.
Asajile anasimulia kivuko kilipopata hitilafu kikiwa katikati ya maji akiwa na gari lake, ilikuwa mithiri ya kile alichokiita kiama.
“Nafanya kazi Posta naishi Kigamboni Machava, nalazimika kuzunguka njia ya darajani, baada ya kukumbwa na madhira ya kivuko, sirudii kupanda nimeizuia hata familia yangu pia,” anasema.
Hakuna ruzuku
Changamoto zote zinazosababisha kudorora kwa huduma, zinachagizwa na uwezo duni wa Temesa kuendesha vivuko hivyo, Mwananchi imebaini.
Uwezo duni huo unasababishwa na mapato yanayotokana na makusanyo ya nauli za abiria wanaotumia vivuko kutotosheleza gharama za uendeshaji.
Pamoja na mazingira hayo, Mmoja wa maofisa waandamizi ndani ya Temesa (jina lake limehifadhiwa), anaiambia Mwananchi kuwa wakala huo unafanya shughuli zake kwa kujitegemea, haupokei ruzuku kutoka serikalini.
Mazingira hayo, anasema yanafanya uendeshaji wa shughuli za wakala, vikiwemo vivuko uwe mzigo.
Kinachotoka Serikali kuu kwa mujibu wa ofisa huyo, ni fedha kwa ajili ya matengenezo makubwa, mishahara ya wafanyakazi wa kudumu na zile za utekelezaji wa miradi mikubwa.
Lakini, anasema matengenezo kinga, ukarabati wa vivuko, gharama za uendeshaji, mishahara ya wafanyakazi wa mkataba ambao ni asilimia 80 ya wafayakazi wote, yote ni jukumu la Temesa.
Vivuko havijitoshelezi
Uchunguzi wa Mwananchi, umebaini katika vivuko vyote 32 vinavyoendeshwa na Temesa nchini, asilimia 95 vinaendeshwa kwa mapato ya vivuko vya Kigamboni-Magogoni.
Kwa maneno mengine, mapato ya baadhi ya vivuko vilivyopo nje ya Dar es Salaam, hayatoshelezi hata kujinunulia mafuta ya dizeli kwa ajili ya kujiendesha.
Kwa maana hiyo, fedha za uendeshaji wa vivuko hivyo hasa cha Pangani, Lindi na Mtwara zinatoka kwenye mapato ya vivuko vya Kigamboni-Magogoni (nyaraka tunazo).
Hali hiyo kwa mujibu wa ofisa wa Temesa aliyeomba hifadhi ya jina lake ili kulinda kibarua chake, inavibebesha mzigo vivuko vya Kigamboni-Magogoni ilhali vyenyewe havina uwezo wa kujibeba.
Mwananchi ilimtafuta, Mtendaji Mkuu wa Temesa, Lazaro Kilahala azungumzia hilo, alisema jukumu la wakala huo ni kuhudumia wananchi sio kufanya biashara.
Kwa sababu ya jukumu hilo, Kilahala anasema juhudi mbalimbali zinafanyika kuhakikisha huduma zinaendelea kuwafikia wananchi na kwa ubora uliokusudiwa.
“Sisi jukumu letu ni kuhudumia wananchi sio kufanya biashara, ndiyo maana kama kuna eneo lina mapato machache tunalazimika mapato ya huku kupeleka kule ilimradi wananchi waendelee kuhudumiwa ndiyo dhamira ha Serikali,” anasema.
Kuhusu vivuko vinavyojiendesha bila kupata faida, Kilahala anasema inatokana na eneo husika na idadi ya abiria.
Anaeleza baadhi ya vivuko vipo katika maeneo yenye abiria wachache, hivyo makusanyo hutokana na idadi hiyo ndogo na kwa sababu wana haki ya kupata huduma, Serikali haina budi kuwapatia.
Nauli hazikidhi uendeshaji
Unakumbuka mara ya mwisho nauli za vivuko zilipandishwa mwaka 2012 na Hayati John Magufuli, wakati huo akiwa Waziri wa Ujenzi?
Magufuli alipandisha nauli hiyo kutoka Sh100 hadi Sh200 ambayo hadi sasa imedumu kwa miaka 12 bila mabadiliko yoyote.
Ingawa kutoongezeka kwake ni faraja kwa wananchi, uchunguzi umebaini kwa upande wa Temesa ni mzigo mwingine, kutokana na ukweli kwamba, gharama za uendeshaji zimeongezeka.
Nauli imebaki kuwa Sh200 ilhali bei ya mafuta, vilainishi na vipuli imeongezeka maradufu, kwa mujibu wa maelezo ya mmoja wa maofisa wa Temesa aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Mazingira hayo, chanzo hicho cha ndani ya Temesa kinasema yanafanya gharama za uendeshaji ziwe zaidi ya kinachokusanywa na hivyo, kusababisha baadhi ya mambo ya msingi yashindwe kufanyika.
“Unachokipata hakitoshi kugharimia uendeshaji, katika mazingira hayo haitawezekana kuwepo kwa huduma zenye ufanisi.
“Wanagoma kuongeza nauli, wanataka huduma bora, hawatoi ruzuku kwa wakala, unadhani ufanisi utatoka wapi?,” kinaeleza chanzo hicho.
Hata hivyo, uchunguzi umebaini kinachokwamisha baadhi ya mambo ikiwemo kuongezwa kwa nauli ni sababu za kisheria.
Kufungua cha 5 cha Sheria ya kuanzishwa kwa Temesa ya mwaka 2005, inamtaja Waziri wa Ujenzi kuwa ndiye mwenye mamlaka ya juu kwa Temesa.
Kwa tafsiri ya sheria hiyo, Waziri wa Ujenzi (Innocent Bashungwa kwa sasa), ndiye mwenye mamlaka ya kupanga nauli za vivuko.
Lakini, Gazeti la Mwananchi linayo nyaraka ya pendekezo la ongezeko la nauli ya vivuko iliyowasilishwa kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wakati huo, (Profesa Makame Mbarawa) na aligoma kuongeza.
Siasa katika biashara
Sababu nyingine ya mkwamo wa kuongezeka kwa nauli ni maslahi ya kisiasa ya viongozi serikalini, kama inavyoelezwa na chanzo kingine ndani ya wakala huo.
“Wanakwambia kule Kigamboni kuna wapiga kura wengi, ukipandisha nauli utawagombanisha viongozi na wananchi wao, kwa hiyo ibaki hivi hivi kwanza.
“Na kwa sababu mwenye mamlaka ya kuamua ongezeko la nauli ni Waziri ambaye kimsingi ni mwanasiasa, anafanya maamuzi yake kwa kuangalia maslahi ya kisiasa sio uhai wa wakala,” anasema.
Alipoulizwa kuhusu nauli, Kilahala alikiri kutoongezeka kwa takriban miaka 12 sasa na kwamba tayari Temesa ilishawahi kwenda kuomba ongezeko hilo.
Lakini, anasema mabadiliko ya nauli hizo yatatokana na tathmini ya kitaalamu ambayo hivi karibuni timu itaundwa kwa ajili ya kuifanya.
“Lakini katika nyakati hizo ni muhimu wananchi waendelee kupata huduma, huku tathmini ikifanyika, hii timu ndiyo itatupa jawabu la kiwango gani kinapaswa kiongezeke,” anasema.
Sea Tax ni mzigo
Ukiachana na kilichoelezwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika ripoti yake ya mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2023, yapo mengine yaliyojificha kuhusu Sea Tax, uchunguzi umebaini.
Ripoti hiyo ya CAG, inabainisha Temesa inalipa Sh5 milioni kila siku kwa Azam Marine Ltd kama gharama ya ukodishaji wa vivuko vya Sea Tax 1 na Sea Tax 2.
Kutokana na gharama hizo, CAG Charles Kichere kupitia ripoti yake hiyo, anasema wakala huo uligharimika kulipa Sh1.8 bilioni kwa mwaka kwa Azam Marine Ltd kwa ajili ya ukodishaji huo kuanzia Julai 1, 2022 hadi Juni 30, 2023.
Kiasi hicho ambacho Temesa imeilipa Azam Marine Ltd ni theluthi moja ya jumla ya mapato ya mwaka yaliyotokana na vivuko vyote vya Kigamboni-Magogoni ambayo ni Sh5.76 bilioni.
Temesa ilibakiwa na Sh3.93 bilioni kwa ajili ya kugharimia uendeshaji ikiwemo mafuta ya vivuko, gharama za kazi, ukarabati na matengenezo na hata hivyo fedha hizo hazikutosheleza mahitaji hayo kwa mujibu wa CAG.
Uchunguzi wa Mwananchi imekwenda mbali zaidi ya ripoti hiyo ya CAG na kubaini, katika kila abiria anayepanda Sea Tax moja (inayobeba jumla ya abiria 250), Temesa inailipa Azam Marine Ltd Sh300.
Temesa inalipa kiasi hicho cha fedha kwa kila abiria anayepanda Sea Tax, ilhali kiasi inachokusanya kwa abiria hao magetini ni Sh200. Kwa maneno mengine inatumia Sh100 kutoka vyanzo vingine kuongezea nauli ya kila abiria anayepanda Sea Tax.
Si hivyo tu, bado Temesa inawajibika kulipa Sh300 kwa kila abiria wakiwemo wanafunzi na maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama, ambao katika mageti hawatozwi nauli yoyote.
Katika mazungumzo yake na Mwananchi kuhusu hilo, Mkurugenzi wa Temesa, Kilahala anasema kukodishwa kwa vivuko hivyo, kulilenga kuongeza huduma, baada ya MV Magogoni kwenda kwenye matengenezo.
“Kwa sababu mahitaji ni makubwa ndiyo maana tumekodi vivuko hivyo, lakini kinachoagaliwa zaidi ni huduma kwa wananchi,” anasisitiza.
Hata hivyo, Mwananchi ilimtafuta Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa azungumzie hayo, alijibu atafutwe Mtendaji Mkuu wa Temesa.
“Mwandishi naomba uwasiliane na Mtendaji Mkuu wa Temesa kwa ufafanuzi zaidi wa maswali yako,” amejibu Bashungwa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi. |
Usalama wa zaidi ya watu 60,000 wanaotumia huduma ya vivuko kuvuka Kigamboni na Magogoni kila siku u | Usalama wa zaidi ya watu 60,000 wanaotumia huduma ya vivuko kuvuka Kigamboni na Magogoni kila siku upo katika mashaka.
Mashaka ya usalama wa watu hao, yanatokana na ubovu wa vivuko hivyo, unaosababishwa na kutofanyiwa matengenezo makubwa kwa mujibu wa sheria, ratiba na matakwa ya kitaalamu.
Hali hiyo inazua hofu ya kuharibika kwa vivuko hivyo vikiwa safarini, kama ilivyowahi kutokea mara kadhaa vyombo hivyo vya usafiri wa majini vilipozima vikiwa na abiria katikati ya maji.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), kwa siku ni zaidi ya abiria 60,000 wanaohudumiwa katika vivuko vya Magogoni-Kigamboni.
Uchunguzi wa Gazeti la Mwananchi, umebaini vivuko hivyo aghalabu hupitiliza muda wa matengenezo makubwa, ambayo ndiyo msingi wa uhai na ufanisi wake.
Sheria ya Usalama wa Vyombo vya Majini (SOLAS) ya mwaka 1974 inataka matengenezo makubwa ya vivuko vinavyotumika kwenye maji ya bahari yasizidi miaka mitano.
Lakini, matengenezo hayo kwa mujibu wa sheria hiyo, pia yanapaswa kufanyika chini ya miaka mitano, kwa maelekezo ya mamlaka ya udhibiti wa huduma za majini ya nchi husika, baada ya kujiridhisha na ubovu wa kivuko.
Mbali na matakwa ya kisheria, taarifa ya ubora wa vivuko (sea worthiness) inaeleza injini za vivuko hivyo (MV Kigamboni, Kazi na Magogoni), zinapaswa kubadilishwa mara tu zitakapofanya kazi kwa saa 10,000.
Ukiukwaji sheria
Katika uchunguzi huo uliofanywa na gazeti hili, umebainika ukiukwaji wa sheria ya SOLAS ya mwaka 1974, kwa kuwa baadhi ya vivuko vinavyotoa huduma Kigamboni vimefikisha miaka sita bila kufanyiwa matengenezo makubwa, huku vikiendelea kufanya kazi na MV Kigamboni ni kimojawapo.
Kwa mujibu wa ratiba ya matengenezo (nakala tunayo), MV Magogoni ilipaswa kufanyiwa matengenezo makubwa mwanzoni mwa mwaka 2023, lakini hadi sasa haijafanyiwa.
Hata hivyo, Mwananchi imearifiwa juu ya Wakala wa Huduma za Meli (TASAC) kusitisha huduma za kivuko hicho kulinda usalama wa watumiaji, lakini bado kipo kazini kinatoa huduma.
“Inashindikana kutekelezeka kutokana na uhalisia wa mahitaji, abiria ni wengi kuliko idadi ya vivuko inalazimika kitumike hivyo hivyo,” anaeleza mmoja wa maofisa wa Temesa, kwa sharti la kutotajwa jina.
Ukiachana na MV Kigamboni, MV Kazi ilifanyiwa matengenezo makubwa mwaka 2022 ikiwa Injini zake zimefanya kazi saa 24,000, ambayo ni mara mbili zaidi ya matakwa ya kitaalamu.
MV Magogoni nayo ambayo kwa sasa ipo katika matengenezo hayo, ilipelekwa Februari mwaka jana, lakini hadi inapelekwa ilishapitiliza muda wa matengenezo kwa zaidi ya miaka mitatu.
Kutokana na hali hiyo, kumekuwa na matukio kadhaa ya vivuko hivyo, kuyumbishwa na upepo kwa urahisi, kadhalika kuzima vikiwa na abiria katikati ya maji.
Januari 25, 2023 kivuko cha MV Kigamboni kilizima katikati ya maji na kulazimika kuvutwa kwa kamba.
Hali kama hiyo, ilitokea Mei 12, mwaka huo kwa kivuko hicho hicho, kadhalika Septemba 18, mwaka huo.
Tatizo ni bajeti
Kutozingatiwa sheria, ratiba na matakwa ya kitaalamu kuhusu matengenezo makubwa ya vivuko hivyo, kunachagizwa na kukosekana fedha za kutekeleza kazi hiyo, kama inavyofafanuliwa na chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Serikali.
Chanzo hicho kilichozungumza na Mwananchi kwa sharti la kutotajwa jina, kinasema matengenezo makubwa ya vivuko hugharimiwa na Serikali kuu kupitia bajeti za mwaka.
Bajeti hizo, anasema aghalabu huwa na vipaumbele lukuki na kutolewa kwake huwa kwa kusuasua.
Mwananchi imelithibitisha hilo kupitia mpango wa matengenezo ya kivuko cha MV Kigamboni unaotaka bajeti yake itolewe katika mwaka huu wa fedha unaoishia Julai.
Licha ya mpango wa matengenezo kutaka hivyo na mwaka huo wa fedha kukaribia mwisho, hakuna kiasi chochote cha fedha kilichotolewa wala mkataba na mkandarasi kusainiwa, (uthibitisho tunao).
“Hakuna fedha ndiyo sababu matengenezo hayafanyiki, mpango upo lakini Serikali ina vipaumbele vingi, hadi matengenezo yafikiwe muda umeshapita,” kinaeleza chanzo hicho.
MV Magogoni kizungumkuti
Kama hiyo haitoshi, masuala hayo hayo ya bajeti yanakwamisha kukamilika kwa matengenezo makubwa ya kivuko cha MV Magogoni.
Kivuko hicho kilipelekwa nchini Kenya, Februari mwaka jana kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo hayo kwa kipindi cha miezi sita yaani hadi Agosti mwaka jana.
Lakini uhalisia tangu kivuko hicho kipelekwe nchini humo, imeshapita miezi 15 bila matengenezo hayo kukamilika na hakina dalili ya kurejea mwaka huu nchini.
Uchunguzi umebaini kuwa, mkwamo huo unasababishwa na Serikali kutokamilisha malipo ya mkandarasi kwa ajili ya matengenezo ya kivuko hicho. Malipo ya awali yaliyopaswa kufanywa tangu Februari mwaka jana, yamefanyika Februari mwaka huu (uthibitisho tunao).
Malipo hayo yaliyofanyika Februari mwaka huu ni asilimia 10 ya malipo yote ya Sh7.5 bilioni ambayo mkandarasi African Marine and General Engineering Company Ltd anapaswa kulipwa.
Ofisa wa ngazi ya juu kutoka kampuni hiyo ya Mombasa nchini Kenya, aliiambia Mwananchi kuwa, hadi sasa ni kazi za awali tu ndizo zilizoanza kufanyika.
Anaeleza matengenezo hayo yalipaswa kuanza mara tu kivuko hicho kilipofika katika karakana, lakini ilishindikana kwa kuwa Serikali ya Tanzania haikuwa imelipa.
“Matengenezo yanahitaji vipuli na vifaa vingine ambavyo African Marine and General Engineering Company Ltd inapaswa kuagiza kwa fedha, kama hakuna fedha iliyolipwa si rahisi kuanza kazi,” anasema ofisa huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Kwa mujibu wa ofisa huyo, malipo ya awali ‘advance payment’ yaliyopaswa kufanyika mwaka jana, ndiyo yamelipwa Februari mwaka huu.
“Kazi zimeanza lakini zile za awali na matengenezo yale yanahitaji kubadilisha kila kitu zikiwemo Injini nne, kwa hiyo hatujafikia hata kuagiza injini, ambao nao ni mchakato unaochukua zaidi ya miezi sita,” anasema.
Kutokana na mazingira hayo, MV Magogoni iliyotarajiwa kurejea nchini, Agosti mwaka jana, haina dalili za kurejea nchini hata mwaka huu utakapoisha.
Temesa yafafanua
Alipoulizwa kuhusu hilo, Mtendaji Mkuu wa Temesa, Lazaro Kalahala anasema shughuli zinaendelea na kivuko kitarejea (bila kuweka wazi ni lini).
Kuhusu kusuasua kwa malipo ya mkandarasi, Mtendaji Mkuu huyo hakuwa tayari kufafanua, akisisitiza Serikali inaendelea kufanya juhudi za kuhakikisha kazi hiyo inatekelezwa.
“Serikali inafanya kila namna kuhakikisha matengenezo yanafanyika ili kivuko kirejee na wananchi waendelee kupata huduma,” anasema.
Alipoulizwa kuhusu vivuko kuchelewa kupelekwa kwenye matengenezo, Kilahala anakiri kuwepo kwa hali hiyo, akifafanua kuwa, inasababishwa na mpangilio wa ratiba bila kuathiri huduma kwa wananchi.
Anaijenga hoja hiyo kwa ufafanuzi kuwa, baada ya kivuko cha MV Magogoni kurejea kutoka kwenye matengenezo (haijulikani ni lini), MV Kigamboni kitapelekwa kupata huduma hiyo.
“Matengenezo yamefanyika kwa kupishana mpango wetu ni kwamba MV Magogoni itakaporudi, MV Kigamboni itakwenda kwenye matengenezo,” anasisitiza.
Meneja wa Ujenzi na Matengenezo ya Vivuko wa Temesa, Lukombe King'ombe anasema kwa sababu mahitaji ya huduma za vivuko ni makubwa, hatua ya kuvipeleka katika matengenezo makubwa inafanyika bila kuathiri huduma hizo.
Kwa sababu ya wingi wa mahitaji, anasema ni vigumu kutoa vivuko vyote kwa pamoja kuvipeleka kwenye matengenezo, inalazimika kupeleka kimoja wakati vingine vikiendelea kuhudumia.
“Kuna idadi kubwa ya watu ambao maisha yao ya kila siku ni kuvuka kwa ajili ya kwenda Kariakoo na Posta kutafuta riziki, hii ndiyo inayofanya tusivipeleke vyote kwenye matengenezo makubwa,” anasema. |
Jumuiya ya wafanyabiashara katika Jiji la Shaoyang nchini China, imesema inalenga kushirikiana na wa | Jumuiya ya wafanyabiashara katika Jiji la Shaoyang nchini China, imesema inalenga kushirikiana na wafanyabiashara wa Tanzania ili kukuza uhusiano uliopo baina ya nchi hizo.
Kadhalika, imedokeza mpango wa kuanzisha ghala la bidhaa zake nje ya nchi, litakalotumika kupokea bidhaa za mitambo na umeme kutoka China kuja Tanzania.
Hayo yameelezwa leo, Mei 23, 2024 na Naibu Meya ya jiji hilo, He Yuan katika kikao chake na jumuiya za wafanyabiashara waliopo nchini.
Amesema pamoja na mambo mengine mkutano huo pia, umelenga kubadilishana mawazo ya biashara na kutambua fursa zilizopo katika masoko ya kimataifa.
Kwa mujibu wa Naibu meya huyo, jiji hilo lipo katika mpango wa kuanzisha ghala nje ya nchi ili kusaidia usafirishaji wa bidhaa za mitambo na umeme na kujumuisha bidhaa nyepesi za viwandani.
"Pamoja na mazao ya kilimo ya Tanzania kama vile asali na chai, bidhaa za walaji kama vile vito na viungo, zote ni sehemu kuu za muunganiko na fursa muhimu za ushirikiano kati ya pande mbili," amesema.
Katika hotuba yake hiyo, amesema kiwango cha biashara kimekuwa kati ya nchi hizo, kutoka Yuan 103,000 (sawa na Sh36 milioni) hadi Yuan milioni 140 (sawa na Sh50 bilioni) ya sasa.
"Idadi kutoka kwa utendaji halisi iliongezeka kutoka 1 hadi 39, bidhaa tatu za juu za kuagiza na kuuza nje zilikuwa za mitambo na umeme, mifuko na masanduku na njiti," amesema.
Kwa upande mwingine, Mkurugenzi Zeing Jianping wa Ofisi ya Biashara ya Manispaa ya Shaoyang ameeleza mipango ya kupanua ghala lao la mtandao nchini.
Amesema mpango huo, unalenga kuleta bidhaa nyingi za Shaoyang katika soko la Tanzania na hivyo kuimarisha mtandao wa biashara ya mtandaoni.
“Tanzania hapa tuna mjumbe, anafanya kazi ya kuwa na ghala Dar es Salaam, hapo baadaye ghala hili kupitia mjumbe wetu litaweza kuleta bidhaa nyingi za Shaoyang Tanzania, hivyo mtandao wa e-commerce na warehouse imekuwa ikipanuka,” alishiriki.
Mkuu wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) wilaya ya Kinondoni, Anthony Mbunda, amesisitiza umuhimu wa jukwaa hilo katika kuwezesha mabadilishano kati ya wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.
"Wafanyabiashara wa China wanapokuja hapa, wanakuja kama wawekezaji. Kama wawekezaji, wanatupa fursa. Sasa tuna faida ya kujifunza kutoka kwao. Wakija wanaleta teknolojia zao, na watu wetu watapata nafasi ya kufundishwa teknolojia hizi,” ameeleza.
Mjasiriamali aliyebobea katika vipodozi vya asili kutoka Ilala, Zaynab Issa, amesema faida za kiuchumi za kusafirisha bidhaa za ndani kwenye masoko ya kimataifa.
"Fikiria kama leo, kama mfanyabiashara, ningeweza kuuza nje bidhaa zangu za ndani kwenye masoko ya kimataifa. Hii ina maana tunakuza uchumi wa nchi. Hata hivyo, pia ni kipengele muhimu kitakachorahisisha ufikiaji wa nyenzo ambazo ni adimu kwetu, na wakati mwingine nyenzo zingine hazipatikani kwao. Hapo ndipo umuhimu wa ushirikiano unapokuja,” anafafanua. |
Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart), umesema Julai mwaka huu, utaanza matumizi ya | Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart), umesema Julai mwaka huu, utaanza matumizi ya mageti ya mfumo wa kadijanja kwa ajili ya abiria watakaopanda usafiri huo.
Kwa mujibu wa Dart, hatua hiyo ni baada ya kukamilika kwa kazi ya kufungwa kwa mfumo wa mageti hayo katika vituo mbalimbali vya mabasi yaendayo haraka, inayoendelea sasa.
Hata hivyo, wakala huo umeweka wazi mpango huo unalenga pamoja na mambo mengine, kudhibiti upotevu wa mapato katika ukusanyaji wa nauli za abiria wa usafiri huo.
Hii si mara ya kwanza kwa Dart kutumia mfumo huo, uliwahi kutumika mwaka 2016 wakati mradi unaanza na huduma hiyo ikisimamiwa nma Max Malipo.
Baadaye mwaka 2018 kadi za kuchanja zilizokuwa zinatumika, zilisitishwa kwa madai kuwa zilikuwa zinavujisha mapato na mfumo wa tiketi ukachukua nafasi.
Hali bado iliendelea kuwa mbaya licha ya mabadiliko hayo, katika mfumo wa tiketi ulibainika wizi wa fedha, kama ilivyowahi kuelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa.
Kutokana na hayo, uamuzi wa matumizi ya kadijanja kupitia mfumo wa mageti umeonekana kuwa muarobaini.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Dart, Ng’wanashigi Gagaga katika moja ya taarifa zake mbele ya waandishi wa habari.
Kwa mujibu wa Gagaga, kadi hizo ni salama na haitakuwa rahisi kudukuliwa.
“Kadi hizi ni salama zaidi si rahisi kudukuliwa zimedhibiti mianya zaidi lakini zina kitu kingine muhimu ndani yake kuna vyumba vingi vya kuweka kadi nyingine kama usafiri wa reli au mabasi yaendayo mikoani,’’ amesema
Hata hivyo, amesema bei ya kadi hiyo itakuwa kubwa tofauti na zile za awali ambazo moja iliuzwa kwa Sh500.
“Bei yake bado hatujapanga lakini tulishashauriwa na Mkaguzi mkuu wa ndani ziuzwe bei juu kidogo badala ya kuuza kwa bei rahisi ili kuzuia watu wasizipoteze kirahisi bado hatujapata bei elekezi,’’ amesema.
Mbali na kuweka salio kwenye kadi hiyo kupitia wahudumu wa mabasi hayo, Gagaga amesema hata kwa simu yako na wakala wa huduma za kifedha inawezekana kulitekelezaq hilo.
“Hatutatumia tena kadi za zamani kwa kuwa ni rahisi zaidi kudukuliwa. Tutatumia mpya kwa waliokuwa nazo tutaweka utaratibu mpya,” amesema.
Awali, akizungumza Dar es Salaam, wakati anafunga mafunzo ya siku tano ya timu ya wataalam 10 wa mfumo wa kadijanja katika kuisanifu na usalama wake, Mkurugenzi wa Dart, Dk Athumani Kihamia amesema tayari wameshaingiza mageti janja zaidi ya 300 yenye thamani ya Sh11 bilioni.
“Mageti haya 300 yamekuja yakiwa na gharama kubwa zaidi ya Sh11 bilioni na wakandarasi wako saiti sasa hivi na asilimia 67 ya kazi imeshakamilika,” amesema Dk Kihamia.
Dk Kihamia amesema mbali na kudhibiti mapato mageti hayo yatasaidia kuokoa muda kwa abiria na kuweka mazingira safi kwa kuacha kutumia karatasi.
Mmoja wa wataalam waliokuwa wanatoa mafunzo hayo kutoka Kampuni ya AdvanIDe, Duncan Chege amesema teknolojia hiyo itakuwa na tija ikianza kutekelezwa kwani ina usalama wa kutosha.
“Tanzania ni nchi ya 50 kwa wao kutoa mafunzo ya teknolojia hiyo lakini Afrika Tanzania ni nchi ya tatu na inatumia teknolojia ya Misifare desire matoleo ya Ev1, Ev2 na Ev3 na mafunzo haya yamezingatia nywila zinazotumika katika kadijanja ,” amesema Dakan
*Mabasi mapya*
Katika hatua nyingine Dk Kihamia amesema kunzia Oktoba mwaka huu Wakala huo utakuwa umepata mabasi mapya 177 ya awamu ya kwanza na kwamba tayari mzabuni ameshapatikana.
“Ifikapo Oktoba mwaka huu tunatarajia kuwa na mabasi mengine mapya 177 mzabuni ameshapatikana na mkataba tunategemea kusaini mwezi huu na tunaamini baada ya miezi mitano utakuwa umetekelezwa,’’ amesema.
Dk Kihamia amesema katika mageuzi hayo bado wanaendelea na mchakato wa awamu ya pili kwa ajili ya barabara inayotokea Mbagala Rangi tatu hadi Mjini kati.
“Mchakato wake umeanza na kufikia mwishoni mwa mwaka huu tunaamini huduma hiyo itakuwa inatolewa kwa barabara ya Mbagala Rangi tatu hadi maeneo mbalimbali ya mjini,” amesema.
Mwishoo.
Kama unadhani msingi wa uponyaji wa maradhi yoyote yanayokusibu ni kununua dawa katika duka la dawa au hospitali unakosea, wakati mwingine hauhitaji kuingia gharama yoyote, ipo tiba uliyoibeba mwilini mwako.
Hivi unajua kuwa kwa kadri unavyocheka, ndivyo unavyoiweka salama afya ya mwili wako dhidi ya athari za magonjwa?
Kwa taarifa yako, ule usemi wa ‘cheka uongeze siku za kuishi’ unaakisi uhalisia, ipo siri ya maisha marefu ndani ya cheko, kama ilivyoelezwa katika Jarida la DailyMail la nchini Uingereza.
Kwa mujibu wa jarida hilo, kucheka ni moja kati ya dawa 20 zilizotajwa na jarida hilo, kuwa na uwezo wa kukuponya bila kulazimika kumeza vidonge kutoka duka la dawa.
Kabla hujaathiriwa na usugu wa dawa dhidi ya vimelea kwa kunywa tembe lukuki za vidonge, cheka utapona, kwa mujibu wa DailyMail.
Mazoezi
Kucheka ni jambo moja, lakini kufanya mazoezi ni jambo lingine ambalo kwa mujibu wa DailyMail, linaimarisha afya ya mwili na akili.
Kadhalika, mazoezi ni dawa kwa magonjwa yasiyoambukiza kama ilivyowahi kuelezwa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Januari mwaka huu alipokuwa katika moja ya maduka ya vifaa vya michezo jijini Dar es Salaam.
“Kumekuwa na ongezeko la kasi la magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari na shinikizo la juu la damu (presha) Watanzania tunatakiwa kuzingatia mtindo wetu wa maisha, kwa kupunguza mafuta na chumvi katika vyakula pamoja na ufanyaji wa mazoezi,” alisema Waziri Ummy.
Kupenda
Jarida hilo limekwenda mbali zaidi na kutaja hatua ya kuwapenda wengine ni dawa muhimu katika maisha ya kila mwanadamu.
Chuki na uadui ni chanzo kikubwa cha tatizo la afya ya akili na hata kufikia hatua ya kudhoofisha mwili, kwani kutopenda wengine husababisha masononeko, yanayochangia kuharibu kwa kiasi kikubwa afya ya akili na mwili.
Upendo ni dawa muhimu kwa kila mtu hivyo ni vyema kupenda wengine na kufurahia mafanikio yao, ili kupunguza mzigo wa chuki moyoni.
Chakula cha asili ni dawa
Si ushamba wala umasikini kula vyakula vya asili kama mihogo, viazi, magimbi, mahindi, korosho na vyinginevyo kwani ni suluhisho la magonjwa yasiyoambukiza kama vile figo, kisukari, moyo, shinikizo la damu, na udumavu.
Kama hiyo haitoshi, DailyMail linataja kufunga ni dawa pia. Ingawa wengi wanatekeleza hilo kama takwa la kiimani.
Mtazamo huo wa jarida hilo, umewahi kuelezwa na Mbobezi wa Magonjwa ya Noyo nchini, Profesa Mohammed Janabi.
Kwa mujibu wa Profesa Janabi, ufungaji wa chakula, kula mara moja au mbili huwa na faida ya kuongeza kinga za mwili na kuongeza maisha.
Usingizi
Wapo baadhi ya watu ambao kulala kwao ni dharula. Kwa taarifa yako, kufanya hivyo kunahatarisha afya yako.
Kwa mujibu wa jarida hilo, kwa kawaida mtu anatakiwa kwa saa nane. Kati ya faida za kulala ambazo hutajwa na wataalamu ni kutuliza ubongo, kufanya ubongo utunze kumbukumbu, ubongo kupata muda wa kufanyia kazi taarifa ulio nazo, mbali na faida kwa ubongo pia husaidia mwili kupumzika na kujijenga upya.
Mwanga wa jua
Yapo maneno na majina mengi ya utani ambayo watu huwapatia wanaopenda kukaa juani, lakini kiuhalisia kufanya hivyo kunaongeza vitamin D.
Imeelezwa kuwa tunahitaji vitamini D, kwa ajili ya miili yetu kufyonza madini ya calcium na fosphati kutoka kwenye chakula, madini yote hayo ni muhimu kwa afya ya mifupa, meno na misuli bila kujali umri wa mtu.
Neno la Mungu
Kusoma na kujifunza neno la Mungu ni dawa, kwa imani mbalimbali watu hufarijika na kujikuta wakiendelea kusonga mbele kutokana na maneno matakatifu ambayo wanayasoma kwenye vitabu vya dini.
Maneno hayo hugeuka dawa kwa afya zao za akili na kufanya wawaze yaliyo mema, hivyo basi faraja na tumaini ambalo hupatikana kutokana na imani ni ngao na dawa kubwa ya afya ya akili na mwili.
Maji
Maji ni dawa ambayo husaidia kuponya magojwa mengi, kwani bila maji ni rahisi kupata matatizo ya ngozi, matatizo kwenye mfumo wa umeng’enyaji, na mengineyo.
Mbali na matatizo hayo, wataalamu mbalimbali wamekuwa wakieleza faida za kunywa maji ambazo hugeuka na kuwa tiba kwenye mwili wa binadamu kwa kusaidia kuponya magonjwa katika mfumo wa mkojo na kurudisha kumbukumbu.
Aidha mtaalamu wa masuala ya lishe kutoka Taasisi ya Chakule na Lishe (TFNC), Julieth Shime, amewahi kusema viungo vingi vya mwili ili viweze kufanya kazi vizuri vinahitaji maji na zaidi ya asilimia 60 ya uzito wa mwanadamu ni maji.
Msamaha
Kujisamehe na kusamehe wengine ni dawa. Kila kukicha yanaibuka matukio ya kikatili ya mtu binafsi kujitoa uhai au kudhuru au kuua wengine, hayo yote hutokana na kushindwa kujisamehe na kusamehe wengine jambo linalosababisha kujenga chuki na kukuza sumu akilini na hapo ndipo yanapoibuka matukio ya kikatili kwenye jamii.
Hivyo dawa kubwa kuepukana na changamoto za afya ya akili ni kuhakikisha mtu binafsi unajisamehe na kisha kuwasamehe wengine waliokukosea.
Marafiki
Marafiki wazuri ni dawa, uliowapa nafasi kuwa karibu kama marafiki ni dawa nzuri kwenye maisha yako lakini pia ni sumu kali inayoweza kukuangamiza mara moja, uchaguzi wa marafiki kwa makini ni jambo la muhimu ili uwapo nao karibu wawe dawa na siyo sumu.
Si hayo tu dawa nyingine zilizotajwa na mtandao huo ambazo hazipatikani dukani na muhimu kwa afya yako ni kujipenda, kutoa shukrani, kuacha kurudia kosa, kutafakari, fikra sahihi, pia kula mboga na matunda.
Kauli ya wataalamu
Mtaalamu wa Afya ya Jamii na aliyekuwa Mkurugenzi wa Kinga, Wizara ya Afya kabla hajastaafu mwaka 2005, Dk Ali Mzige anasema hakuna dawa kwa kila ugonjwa au maradhi.
“Kifanye chakula chako kiwe dawa yako, ifanye dawa yako iwe chakula chako. Waislamu wana fundishwa fungeni mwezi wa Ramadhan mtapata siha yaani afya na Wakristo hufunga kipindi cha Kwaresma. Unapofunga seli za saratani zina kosa sukari ya kuzifanya ziwe hai,” anasema.
Anafafanua kuwa seli za saratani hazipendi hewa ya oksijeni, kwa mtu anayefanya mazoezi ya kukimbia hewa safi ya oksijeni inauwa virusi na bakteria.
Dk Mzige anasema mtu anapofunga lehemu au cholesterol zina pungua, zile mbaya zinazotengenezwa na nyama tunazokula kupita kiasi na kwamba lehemu nzuri hutengeneza homoni na kuimarisha kinga.
“Unapotimiza tendo la ndoa kwa ufanisi, shinikizo la damu hupungua na mwili unapata kupumzika kimwili na kiakili. Unapofanya kitu kizuri moyo wako unakuwa na faraja. Ukinuna unakosa usingizi na utakula zaidi kupunguza msongo wa mawazo, kumbe ndio unazidisha,” anasema Dk Mzige.
Profesa wa sayansi ya neva na ile ya saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha California, Berkeley, Mathew Walker alichunguza takwimu kutoka kwa mamilioni ya watu ambao wamehusika katika utafiti wa tawi la sayansi iliyotafiti visa, usambazaji na udhibiti wa magonjwa na sababu nyingine zinazohusiana na afya.
“Iwapo una hamu ya kutaka kuishi maisha marefu basi utalazimika kuwekeza katika kujipatia usingizi mzuri,” alisema.
Utafiti ulibaini binadamu anapolala, ubongo wake hupata wakati wa kutunza kumbukumbu na kufanyia kazi taarifa ulizonazo ambayo ni matukio ya kutwa nzima au kipindi ambacho binadamu alikuwa ameamka.
“Ni muda ambao sumu au uchovu huondoka katika mwili na kuuruhusu kufanya kazi vizuri utakapoamka,” alisema Profesa Mathew na kuongeza kuwa iwapo hupati usingizi waone wataalamu wa afya. |
Serikali imesema ipo katika hatua ya kuainisha mahitaji, sifa na aina ya teknolojia zinazohitajika k | Serikali imesema ipo katika hatua ya kuainisha mahitaji, sifa na aina ya teknolojia zinazohitajika katika sekta mbalimbali na kuweka muda maalum kwa ajili ya kupatikana.
Hatua hiyo kwa mujibu wa Serikali, inalenga kuhakikisha sayansi na teknolojia inapewa kipaumbele katika maendeleo ya rasilimali watu na ubunifu.
Katika utekelezaji wa hilo, vyombo vya habari vimetajwa kuwa muhimili muhimu wa kuelimisha na kuibua habari mbalimbali zenye lengo la kuhamasisha ubunifu kama inavyoelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited (MCL), Bakari Machumu.
Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam leo Jumatatu, Mei 20, 2024 na Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Ladislaus Mnyone katika warsha kwa wahariri na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya 10 ya wiki ya ubunifu.
Amesema maandalizi hayo ya mpango wa taifa wa teknolojia, utasaidia nchi na wadau kuwekeza katika maeneo ambayo Serikali itakuwa imeyaainisha.
"Hii inafanyika kwa makusudi ili sasa hata haya mabadiliko ya mitalaa na sera yaunganishwe na mahitaji yetu ya nchi katika sayansi na teknolojia," amesema.
Sambamba na maandalizi ya mpango huo, amesema mkakati mwingine wa kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali watu yenye ubunifu, Serikali inatafuta namna ya kuwatumia Watanzania waliopo nje ya nchi.
“Kwa sasa tunatafuta namna ya kuwatumia diaspora ili wasaidie katika kukuza ubunifu, sayansi na teknolojia. Tunajua wengine wana uraia wa mataifa mengine, lakini tunachokifanya ni kuhakikisha tunawatumia,” amesisitiza.
Mpango mwingine wa kuhakikisha kunakuwa na rasilimali watu yenye ubunifu, amesema kuwatumia wafanyakazi waliopo katika taasisi lakini uwezo wao wa kufikiri ni zaidi ya kazi wanazofanya.
“Kama nchi ni muhimu kuona namna ya kuwatumia watu hao ili kuendana na mahitaji ya Sayansi na Teknolojia,” alisema.
Katika kufanikisha upatikanaji wa rasilimali hiyo, ameeleza
Kuhusu juhudi za Serikali, Profesa Mnyone mabadiliko ya mfumo wa elimu yamefanyika, rasimu ya mkakati wa matumizi ya Tehama imekamilika na vituo vya umahiri vimeanzishwa kuzalisha wabunifu kuendana na mahitaji ya nchi.
Machumu
Hata hivyo, ufikiwaji wa mlengo hayo, unahitaji mchango wa vyombo vya habari, katika kuelimisha, kuibua na kuandika habari zitakazoshawishi umma kuvutiwa na ubunifu, kwa mujibu wa Machumu.
Katika hotuba yake, Machumu amesema ni muhimu kwanza wanahabari na vyombo vyao viwezeshwe ujuzi na uwezo ili vinaposikia habari kuhusu ubunifu viitazame kwa picha kubwa.
Kadhalika, amesisitiza umuhimu wa kujenga ubobevu kwa wanahabari ambao kimsingi watakuwa na ujuzi na maarifa mapana kuhusu masuala ya ubunifu.
"Katika kulitekeleza hilo, ni muhimu kuwepo wanahabari waliobobea katika habari za masuala ya ubunifu ili inapotokea aina hiyo ya habari waitazame kwa picha kubwa," amesema.
Sambamba na hilo, amependekeza kuwepo ushirikiano kati ya vyombo vya habari na asasi za kiraia na wadau wengine na wawezeshe uandishi wa habari za ubunifu kwa wanahabari.
“Kama ni mwelekeo wa Serikali kuna umuhimu wa kutengeneza ushirikiano na vyombo vya habari kwa maana ya kuvielimisha na kuwezesha waandishi wakaripoti habari kuhusu ubunifu,” amesema.
Hata hivyo, amesema uwezekano wa hayo utatokana na vyombo hivyo vya habari kupewa uhuru wa kutekeleza jukumu hilo.
Ametaka kuwepo mkakati wa mawasiliano utakaohusisha kuwajengea uwezo wanahabari ili wabobee katika uandishi wa habari za ubunifu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk Amos Nungu amesema pamoja na kuwepo bunifu mbalimbali, zipo zinazoshindikana kuendelezwa kwa sababu ya kukosa soko.
Kwa mujibu wa Dk Nungu, baadhi ya bunifu zinavutia machoni, lakini kiuhalisia hazina soko kwa Tanzania, hivyo kuna haja kwa wabunifu kuzingatia wanabuni kitu chenye walaji.
Meneja wa Mipango wa mradi wa Fungu chini ya Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Joseph Manirakiza amesema katika wiki hiyo yatashuhudiwa mageuzi ya nguvu katika maendeleo ya ubunifu.
“Baada ya wiki hiyo kuzinduliwa Dar es Salaam, tunatarajia wiki ijayo kwenda Tanga kuhitimisha,” amesema. |
Helikopta iliyokuwa imembeba Rais wa Iran, Ebrahim Raisi imeanguka baada ya kupata shida katika kutu | Helikopta iliyokuwa imembeba Rais wa Iran, Ebrahim Raisi imeanguka baada ya kupata shida katika kutua.
Kwa mujibu wa televisheni ya Taifa ya Iran, helikopta hiyo imeanguka leo, Mei 19, 2024 karibu na Mji wa Jolfa, uliopo mpakani na taifa la Azerbaijan.
Hata hivyo, taarifa hiyo haijaweka wazi chanzo cha moja kwa moja cha ajali hiyo, ingawa imearifiwa mkuu huyo wa nchi alikuwa safarini katika Mkoa wa Azerbaijan Mashariki wa Iran.
Waokoaji wanasema walijaribu kufika eneo la tukio, lakini hali ya mvua kubwa iliyokuwa inanyesha eneo hilo, ilikwaza jitihada zao, kwa mujibu wa ilivyoripotiwa katika televisheni ya taifa hilo.
Bado haijawekwa wazi kuhusu athari zilizosababishwa na ajali hiyo na hata afya ya kiongozi huyo mkuu wa taifa la Iran haijabainishwa.
Lakini wanaodaiwa kuwepo katika helikopta hiyo ni Raisi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amirabdollahian, Gavana wa Azerbaijan Mashariki Malek Rahmati na Mwakilishi wa Viongozi Wakuu wa Iran Mashariki mwa Azerbaijan, Ayatollah Ale-Hashem.
Raisi alikuwa nchini Azerbaijan leo kuzindua bwawa na Rais wa taifa hilo, Ilham Aliyev ikiwa ni la tatu kujengwa na mataifa hayo mawili kwenye Mto Aras.
Iran inaendesha aina mbalimbali za helikopta nchini humo, lakini vikwazo vya kimataifa vinafanya iwe vigumu kupata aina ya ndege hizo.
Kiongozi huyo anakabiliwa na vikwazo kutoka Marekani kutokana na kinachodaiwa kuwa, amehusika katika mauaji makubwa ya maelfu ya wafungwa wa kisiasa mwaka 1988 mwishoni mwa vita vya umwagaji damu vya Iran na Iraq.
Kabla ya wadhifa huo, aliwahi kuiongoza mahakama ya nchi hiyo na ndiye anayetabiriwa kuwa mrithi wa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei.
Raisi alishinda uchaguzi wa rais wa Iran wa 2021, ulioshuhudiwa kuwa na idadi ndogo ya wapiga kura katika historia ya Jamhuri ya Kiislamu.
Chini ya Raisi, Iran sasa inarutubisha uranium katika viwango vya karibu vya kiwango cha silaha na kukwaza ukaguzi wa kimataifa. |
Tuhuma za kughushi nyaraka, uchepushaji wa makusanyo ya Serikali na ubadhirifu wa fedha za umma, zim | Tuhuma za kughushi nyaraka, uchepushaji wa makusanyo ya Serikali na ubadhirifu wa fedha za umma, zimekiweka katika mashaka kibarua cha Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Juma Hamsini na wenzake.
Mashaka hayo, yanatokana na amri ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda aliyemwagiza Katibu Tawala wa mkoa huo, Missaile Mussa awasimamishe kazi watumishi hao kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo dhidi yao, unaofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Mzizi wa tuhuma hizo ni hoja iliyoibuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Utalii Tanzania (Tato), Wilbard Chambulo akiwatuhumu watumishi hao katika Jiji la Arusha.
Miongoni mwa tuhuma zilizoibuliwa naye ni utengenezaji wa nyaraka bandia na kuchepusha baadhi ya makusanyo ya kodi, jambo lililomlazimu Makonda kuagiza uchunguzi wa Takukuru.
Tuhuma kama hizo ziliwahi kuibuliwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo dhidi ya Mkurugenzi wa wakati huo, Dk John Pima mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na hivyo alisimamishwa kazi.
Pima na wenzake wawili Februari 16, 2023 walishinda rufaa waliyokata kupinga adhabu ya kifungo cha miaka 20 waliyokuwa wamehukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.
Machi 20, 2024 Pima na wenzake watatu walifutiwa kesi na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) na kuwafungulia kesi nyingine mbili za uhujumu uchumi ambazo bado zinaendelea.
Hayo yalijiri jijini Arusha juzi, katika kikao cha Makonda na wadau wa utalii, kilicholenga kusikiliza na kutatua changamoto za sekta hiyo katika Mkoa huo.
Ilivyokuwa
Katika kikao hicho, Chambulo alionyesha nyaraka alizodai zinathibitisha matendo maovu ya watendaji wa Jiji hilo.
Katika ukarasa wa kwanza wa fomu aliyopewa na halmashauri hiyo, alisema imeandikwa jina la kampuni yake, lakini namba za biashara na utambulisho sio zake.
Pamoja na mazingira hayo, alisema watumishi hao walimpa namba ya malipo kwa ajili ya kulipia ushuru wa biashara uliopaswa kuwa Sh19 milioni ambao ni asilimia 0.3 ya pato ghafi.
Alieleza kushangazwa na fomu aliyopewa na halmashauri yenye taarifa tofauti na fomu halisi aliyoijaza na kuikabidhi kwao.
“Hii nyaraka siyo ya kwangu nyaraka niliyojaza ni hii hapa na mhuri wangu nimepiga, huyu alipata wapi jina linaitwa The Tanganyika Wilderness Camps, ukifungua hapa kwenye nyaraka ya halmashauri hii hapa (anaonyesha).
Ukiangalia vizuri namba ya mlipaji hii siyo hata namba ya kwetu, hata tarakimu za simu imepungua moja kwa hiyo imebandikwa, yangu hii hapa (akionyesha ukurasa wa kwanza wa fomu hizo) ,” alisema.
Mbele ya kikao hicho, Chambulo alieleza hata utambulisho wa biashara unaoonekana katika fomu hiyo umejazwa tofauti na kampuni yake, jambo aliloshuku kwamba pengine kodi haziendi kunakostahili.
“Hii inatuogopesha kwani tunasikia kule Mbeya wanaiba, huku ukisikia wanaiba na sisi wafanyabiashara tusikubali mtu ale hela,” alieleza.
Mkurugenzi
Awali, akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Jiji hilo, Hamsini alielezea utekelezaji wa maelekezo aliyopewa na Makonda katika kikao cha kwanza cha Aprili 13, mwaka huu.
Katika kikao hicho cha awali, Chambulo aliibua tuhuma za kutozwa ushuru wa huduma kiasi cha Sh24 milioni, lakini risiti aliyopewa iliandikwa amelipa Sh3.6 milioni.
Hata hivyo, baada ya tuhuma hizo Chambulo, Hamsini alifanya mkutano na vyombo vya habari na akisema madai ya mfanyabiashara huyo ni uongo mtupu.
Makonda
Baada ya kusikiliza maelezo ya mfanyabiashara huyo, Makonda aliagiza Takukuru kuanza uchunguzi dhidi ya watendaji wa halmashauri hiyo na wote wanaotajwa kuhusika na tuhuma hizo kusimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi huo.
Katika kuwasimamisha kazi, alimwagiza Katibu tawala wa Mkoa huo, kulitekeleza hilo.
“Ni utovu wa nidhamu uliopitiliza kutoka kwenye kikao cha kiongozi wako amekupa maelekezo kaunde timu ya kitaalamu mpitie hoja waite TRA, Tato na wadau wengine kaeni pitieni hoja angalieni sheria leteni mapendekezo, ila unakwenda kufanya press conference (mkutano na waandishi wa habari.
“Wale wote wanaohusika leo watachukuliwa na Takukuru, mfumo wote wa malipo uchunguzi utaanza leo kwa amri yangu ili tujue huyu anayepokea hela kwa ‘code number’ inayotofautiana na code namba ya kampuni husika, huyu anayepokea hela ambaye ameweka namba ya simu hata hazijakamilika halafu majina ni ya watumishi ambao wanatoka kwenda kukamata wafanyabiashara kwa mgongo wa kukusanya kodi ya Serikali kumbe inawezekana ni mfumo unaingiza hela kwa watu wengine,” aliongeza.
Takukuru
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mkuu wa Takukuru mkoa wa Arusha, Zawadi Ngailo alisema tayari uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo umeshaanza na kwa sasa wapo katika hatua ya mahojiano.
“Tumeshaanza mahojiano na tutahoji watumishi wote wa kitengo kinachohusiana na ukusanyaji wa mapato na watumishi wengine kwa kadri tutakavyohitaji taarifa, kwa sasa ni mapema mno kujua mtuhumiwa ni yupi ila tunatarajia hadi mwisho wa wiki tutajua nani mtuhumiwa na nani ni nani,” alisema. |
Hali imeendelea kuwa ngumu katika ufaulu wa mtihani wa leseni ya Baraza la Famasia Tanzania kada ya | Hali imeendelea kuwa ngumu katika ufaulu wa mtihani wa leseni ya Baraza la Famasia Tanzania kada ya watoa dawa na fundi dawa wasaidizi, baada ya robo tatu ya wanafunzi kufeli.
Katika mtihani huo uliohusisha watahiniwa 200, wanafunzi 184 wameshindwa kufaulu katika awamu ya kwanza, hivyo baadhi yao wametakiwa kurudia mtihani huku wengine wakitakiwa kurudia darasa.
Hii si mara ya kwanza ufaulu duni kushuhudiwa katika mtihani wa kada hizo, iliwahi kutokea katika matokeo ya Oktoba mwaka jana, ambapo asilimia 61.2 walilazimika kurudia mtihani na wengine asilimia 23.3 wakirudia darasa.
Hali mbaya ya ufaulu ilitokea hata katika mtihani wa Aprili mwaka jana, kati ya watahiniwa 1,618 ni 514 pekee ndiyo waliofaulu, wengine waliangukia kurudia mitihani na baadhi kurudia darasa.
Taarifa ya matokeo hayo, imetolewa leo Ijumaa Mei 17, 2024 na Baraza la Famasia Tanzania, ikionyesha mwendelezo wa anguko la ufaulu wa wanafunzi katika mtihani huo.
Katika taarifa hiyo, wanafunzi 49 wa kada ya watoa dawa waliofanya mtihani huo, ni watatu pekee ndiyo waliofaulu, 35 wakitakiwa kurudia mtihani na 11 wamefeli kabisa.
Kwa upande wa kada ya fundi dawa saidizi iliyokuwa na watahiniwa 151, waliofaulu ni 13, wengine 105 wametakiwa kurudia mtihani na33 wakifeli kabisa.
Matokeo yaliyofutwa
Sambamba na ufaulu duni, matokeo ya mtihani wa fundi dawa sanifu yamefutwa kutokana na udanganyifu.
Hatua ya kufutwa kwa matokeo hayo, imetokana na kile kilichoelezwa na baraza hilo kuwa, ilithibitika kufanyika udanganyifu katika mitihani yote mitatu baada ya kikao cha baraza cha Mei 11.
“Matokeo hayo yamefutwa kwa mujibu wa kanuni Na. 31(2) (a) ya kanuni ya elimu na mafunzo (The pharmacy (Education and Training Regulations), 2005 G.N. No. 333 ya 2005 na Sehemu ya 11 (c) ya Mwongozo wa Mitihani ya Taaluma na Usajili,” imeeleza taarifa ya baraza hilo.
Msingi wa hatua hiyo, ni kile kilichoelezwa na baraza hilo kuwa, linalenga kuwa na wanataaluma wenye sifa na weledi, kulinda afya na usalama wa wagonjwa.
Hata hivyo, imeelezwa wanafunzi waliofutiwa matokeo hayo, wanapaswa kurudia mitihani hiyo Julai 16 hadi 18, mwaka huu bila malipo.
“Vituo vya mitihani vitakuwa kama walivyopangiwa hapo awali na namba mpya za mitihani watatumiwa hivyo hawatahitajika kujisajili tena kwenye mfumo," limeeleza baraza hilo.
Kutokana na matokeo hayo, Sylvester Maxwell kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X ameandika tatizo ni wanaodahiliwa kusoma fani hiyo na nyingine hawana uwezo.
Nyombi naye kupitia mtandao huo, ameandika "kutokana na upungufu mkubwa wa wataalamu wa afya 'focus' imekuwa kwenye namba (quantity), sasa ni muhimu kuweka msisitizo kwenye ubora (quality). Hii ni changamoto mtambuka." |
Umewahi kupangiwa mtindo wa maisha kwa masharti ya mkataba wa nyumba ya kupanga unayoishi au uliyowa | Umewahi kupangiwa mtindo wa maisha kwa masharti ya mkataba wa nyumba ya kupanga unayoishi au uliyowahi kuishi?
Swali hili linaakisi uhalisia wa karaha, vituko na maajabu ya masharti yaliyopo kwenye mikataba ya nyumba za kupanga yanayowakumba Watanzania wengi.
Masharti hayo kwa mujibu wa baadhi ya wapangaji, yanalazimu kubadili mtindo wa maisha na wakati mwingine kuenenda itikadi ambazo ni kinyume na asili yako.
Wapo waliokwenda mbali zaidi, wakieleza masharti ya mikataba hiyo yamewahi kuwaondoa kwenye nyumba siku chache baadae ya kuhamia, wakiacha kodi za miezi kadhaa.
Kuzaa ni wajibu na haki ya binadamu, lakini kwa baadhi ya nyumba ni haramu kwa mujibu masharti ya mikataba yake, kama inavyosimuliwa na mmoja wa wapangaji, daddys_heart kupitia mtandao wa Instagram.
"Hataki mtoto (mwenyenyumba), sasa nimpeleke wapi, ndani mwisho watu watatu," aliandika daddys akijibu swali lililoulizwa katika ukurasa wa Instagram wa Mwananchi_official linalohoji 'Umewahi kukutana na sharti gani la ajabu kwenye mikataba nyumba za kupanga.'
Ukistaajabu ya daddys, yaliyomkuta auntyabdallahrava yatakushangaza, aliyekutana na sharti linalokataza mpangaji kupokea wageni, eti watajaza choo.
Sashajacob naye alikutana na sharti la kutoruhusiwa kuhusiana kimapenzi na mpangaji mwenziwe.
Marufuku ya kuingiza mwanamke zaidi ya mmoja, kula kitimoto, miguno kusikika wakati wa tendo la ndoa na hata kuwasha redio kwa sauti kubwa, ni masharti mengine kero yaliyoibuliwa na wapangaji.
Licha ya kulalamikiwa kuweka masharti magumu katika mikataba ya nyumba zao, wamiliki wa nyumba hizo, wanasema ili kuyaepuka masharti jenga nyumba yako.
"Kama wanaona masharti magumu wajenge za kwao, nyumba yangu mimi ndiye ninayeweka masharti," anasema Mzee Lilla anayemiliki nyumba ya wapangaji jijini Dar es Salaam.
Wapangaji
Ilikuwa ngumu kwa Lavina Joseph kuishi kwenye nyumba ambayo, pamoja na mambo mengine inakatazwa kutandika shuka jekundu, leupe na kupika pilau.
Kwa mujibu wa Levina, katazo hilo halikutoka mdomoni mwa mwenyenyumba bali ni sharti la mkataba wa moja ya nyumba za kupanga Tegeta, Dar es Salaam.
Sambamba na sharti hilo, Levina anaeleza kustaajabishwa na sharti la wapangaji kuepuka kuringishiana wenza, alilolikuta katika nyumba ya kupanga Mbezi Beach, jijini humo.
"Nilipouliza wakanambia kuringishiana kulikomaanishwa ni ile tabia ya leo upo na huyu umeachana naye, kesho na yule unaachana naye keshokutwa mwingine," anasema.
Juma Abdallah alishindwa kumaliza miezi sita katika nyumba ya kupanga Mabibo, Dar es Salaam, baada ya kulazimishwa awe na uhusiano wa kimapenzi na mtoto wa mwenyenyumba.
"Nilikuwa nikimleta mwanamke wangu, yule mama anakaa sebuleni anaimba nyimbo za ajabu, kila muda ananiita. Mwisho wa siku akanambia nitembee na mwanawe na sio wanawake wengine," anasema.
Ingawa halikuwa sharti la mkataba, Juma anasema alilazimika kuhama kutokana na vituko alivyoonyeshwa na mwenyenyumba huyo.
Pamoja na wapangaji kuwa na mita yao, mwenyenyumba wa Rehema Kassim aligoma kuwaruhusu wajinunulie wenyewe umeme.
Badala yake, katika mkataba wa nyumba yake, ameweka sharti la kila mpangaji kumpa Sh15,000 kwa ajili ya umeme kwa mwezi, hiyo ni tofauti na kodi.
"Wapangaji tuna mita yetu, lakini mwenyenyumba analazimisha hela ya umeme tumpe yeye ndiyo atununulie. Ukimwambia tukusanye wenyewe anatwambia tujenge nyumba zetu.
"Kuiomba risiti ya luku hataki kutuonyesha, tunalipa hizo hela tupo wapangaji 10 lakini umeme unaisha kabla ya nusu mwezi," anasena Rehema.
Katika nyumba nyingine, mpangaji hana ruhusa ya kuwa na baadhi ya vifaa vya umeme likiwemo jokofu.
Kwa mujibu wa Suzan Setao, kwenye nyumba anayoishi hawaruhusiwi kutumia jokofu na hilo ni moja ya masharti ya mkataba.
"Mwenyenyumba anasema jokofu linamaliza umeme kwa hiyo hatutumii na anakuja kukagua kama limewashwa au laa," anasema.
Wenye nyumba
Katika maelezo yake Mzee Lilla, anasema namna pekee ya kuepuka masharti ni kujenga nyumba yako.
"Mimi kibanda changu (nyumba) sio cha urithi, nilipambana mwenyewe nikajenga, kwa hiyo naweka masharti kulinda nyumba yangu, mpangaji ni mtu wa kupita usipokuwa mkali ataharibu kisha anaondoka," anasema.
Kwa mujibu wa Mzee Lilla, kwa watu hasa vijana wenye uelewa masharti hayo wanapaswa kuyageuza changamoto na wawe na shauku ya kujenga nyumba zao.
Aurelia Kimaro mmiliki mwingine wa nyumba Magomeni, Dar es Salaam, anasema tabia za wapangaji ndizo zinazochagiza wenyenyunba waweke masharti magumu.
"Kweli ukimpangisha mtu chumba kinakuwa chini ya himaya yake, lakini kwa sababu wewe ndiye unayejulikana chochote atakachokifanya aibu ni kwako.
"Unakuta mpakangaji kila siku analeta mpenzi mpya, nyumba inageuka danguro. Ili kuyaepuka hayo unaweka masharti mapema," anasema.
Ni janga kwa saikolojia
Mwanazuoni aliyebobea katika Saikolojia, Dk Chriss Mauki
Mtazamo wa kisheria
Licha ya masharti hayo, Mtaalamu wa sheria, Patience Mlowe anasema mara nyingi wapangishaji hawafuati masharti ya kisheria.
Anaeleza upangishaji ni biashara rasmi na inatambulika kisheria, chini ya sheria ya ardhi ya mwaka 1999 na ndani yake imeeleza nini kinampasa mpangaji na mpangishaji na namna mkataba wa nyumba ya kupanga inavyopaswa kuwa.
"Kwa kawaida wanaofuata sheria ni wale wapangishaji wa nyumba kubwa kama maghorofa na apartments, hawa wa nyumba za kawaida wanaishia kwenye mikataba wanaypandikiana wenyewe," anasema.
Hata hivyo, sheria hiyo kuanza Ibara ya 88 inaweka wazi haki za mpangaji, ikiwemo kukaa kwenye nyumba kwa muda aliolipa bila kubughudhiwa.
Matakwa mengine kwa mujibu wa sheria hiyo ni mpangaji kukaa kwenye nyumba ambayo ina uhakika wa ubora, iwapo kutatokea hali tofauti mwenye nyumba anapaswa kuirekebisha.
Hata hivyo, sheria hiyo inatambua kuhusu makubaliano ya mpangaji na mpangishaji ingawa yenyewe imeweka masharti ya jumla. |
Baada ya kupotea kwa siku nne mfululizo, hatimaye huduma ya intaneti imerejea, huku ikiacha maumivu | Baada ya kupotea kwa siku nne mfululizo, hatimaye huduma ya intaneti imerejea, huku ikiacha maumivu kwa watumiaji, wakiwemo madereva wa taksi mtandao, vyombo vya habari, benki na mawakala.
Kwa siku nne hizo, intaneti ambayo ndiyo msingi wa baadhi ya huduma muhimu za mtandaoni, ilikosekana nchi nzima na kusababisha mkwamo wa shughuli mbalimbali.
Huduma hiyo ilikosekana kuanzia asubuhi ya Mei 12, mwaka huu na kudumu hadi jana, ambapo wananchi walishuhudia mabadiliko ya upatikanaji wa intaneti.
Kampuni mbalimbali za mitandao ya simu, zilichapisha taarifa ya kufurahia hatua ya kurejea kwa huduma hiyo, ambayo awali ilikwazwa na kukatika kwa mkongo wa mawasiliano baharini wa SEACOM na EASSy kati ya Msumbiji na Afrika Kusini.
Sambamba na taarifa hiyo, kampuni ya Vodacom ilikwenda mbali zaidi na kuahidi kurudisha vifurushi vya wateja wake, vilivyopotea bila kutumika katika kipindi cha changamoto hiyo.
Mbali na kampuni hizo, hakikisho la kurejea kwa huduma hizo, lilitolewa pia na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye bungeni jijini Dodoma.
Taarifa za mitandao
Kutokana na hali hiyo, kampuni ya mtandao wa simu ya Vodacom kupitia taarifa yake kwa umma jana, ilitangaza kuwarudishia wateja wake vifurushi hivyo.
“Tunaelewa tukio hili limeleta usumbufu, tunaomba radhi kwa hilo. Kwa sababu hii, wateja wote walioshindwa kutumia huduma ya intaneti watarejeshewa vifurushi vyao. Tunaendelea kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha unapata huduma bora na kasi ya juu kabisa,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire amesema, "sisi tutoe shukrani zetu kwa watoa huduma walioshirikiana nasi kurejesha huduma."
Airtel
Kampuni ya mtandao wa simu wa Airtel nayo katika taarifa yake, ilieleza kurejea kwa intaneti, baada ya juhudi za wataalamu waliokuwa wakifanya kazi usiku na mchana.
“Ingawa tumefanikiwa kurejesha huduma inawezekana kukawa na changamoto kadhaa. Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa uvumilivu mliouonyesha,” imeeleza taarifa hiyo.
Nape kuhusu kurejea kwa mtandao
Akizungumza bungeni jijini Dodoma jana, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alitangaza hali ya kurejea kwa upatikanaji wa intaneti kwa asilimia 80 na kwamba hadi mchana wa jana hali ingeridhisha zaidi.
"Tulikuwa tukipitia changamoto kubwa ya upatikanaji wa mtandao, hivi tunavyozungumza upatikanaji upo zaidi ya asilimia 80, tunatarajia leo (Mei 15, 2024) kufikia mchana tutakuwa tuko katika hali nzuri" alisema Nape.
Kauli hiyo ya Nnauye ilitokana na mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Makete, Festo Sanga aliyetaka hatma ya mchakato wa uombaji wa ajira za Jeshi la Polisi, uliotatizwa na kukosekana kwa intaneti.
Hata hivyo, suala hilo lilijibiwa pia na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni aliyesema katika mchakato wa maombi hayo, siku tano zimeongezwa. |
Hatma ya nani na nani watakaoteuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwania nafasi z | Hatma ya nani na nani watakaoteuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwania nafasi za uenyekiti wa kanda, inatarajiwa kujulikana katika siku tatu zijazo kuanzia Jumamosi hadi Jumatatu.
Pamoja na kujulikana kwa wateule hao, ndani ya siku hizo tatu ndipo msimamo wa chama hicho kuhusu kauli ya Makamu Mwenyekiti wake Bara, Tundu Lissu unapotarajiwa kuwekwa bayana.
Katika siku hizo Chadema inatarajiwa kufanya kikao cha Kamati Kuu, ambacho pamoja na mambo hayo mawili, pia kitabeba ajenda za hali ya kisiasa, kufutwa kwa uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti mkoani Njombe, maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa na tathmini ya maandamano yaliyofanyika hivi karibuni.
Kiu ya wengi kutoka kwenye kamati kuu hiyo ni mrejesho wa chama hicho juu ya kauli ya Lissu ya Mei 2, mwaka huu mkoani Iringa, aliyodai uwepo wa fedha zilizomwagwa kwenye uchaguzi wa ndani wa Chadema.
Katika hotuba yake siku hiyo Lissu alisema: “Wakati nakuja hapa Iringa jana na juzi kulikuwa na mtafaruku mkubwa sana, sijui kama mnafahamu, ndani ya chama chetu kuna pesa nyingi ajabu kwenye uchaguzi huu.
“Leo kwenye uchaguzi kuna hela ya ajabu, ninyi mnafikiri hiyo hela ni ya wapi? Mnafikiri hiyo hela ni ya nani? Mnafikiri hiyo hela itatuacha salama? Ukitaka kujua kwamba hatuko salama, fuatilia mitandaoni,” alisema Lissu.
Gazeti hili jana limethibitishiwa juu ya ajenda za kikao hicho na chanzo cha kuaminika ndani ya chama hicho, kilichoeleza: “Itakutana jijini Dar es Salaam kwa siku tatu kuanzia Jumamosi na kumalizika Jumatatu. Kisha maazimio ya kamati kuu yatatolewa kwa umma na mwenyekiti (Freeman Mbowe).”
Licha ya ajenda ambazo Mwananchi limethibitishiwa kuwepo katika kamati kuu hiyo, taarifa rasmi ya Chadema imezitaja ajenda za kupokea taarifa ya chaguzi katika ngazi mbalimbali za chama, tathmini ya maandamano na usaili na uteuzi wa wagombea wa kanda ndizo zitakazojadiliwa.
Hata hivyo, mwaliko kwa wanachama wote waliochukua fomu za kuwania nafasi hizo katika kanda za Nyasa, Serengeti, Victoria na Magharibi, umetolewa ukiwataka kuwepo Dar es Salaam kuanzia Mei 11, mwaka huu.
Mashaka ya makada
Kauli ya Lissu, imeibua mashaka ya makada wa chama hicho mkoani Mbeya, wakisema hawana uhakika iwapo watashiriki uchaguzi huo kwa kutokana na kauli tata za viongozi.
Rehema Chamila ni kada wa chama hicho, alisema pamoja na ukereketwa wake, haoni tena sababu ya kushiriki uchaguzi huo kwa kuwa unaingiliwa na mambo mengi.
“Kwa sasa sioni sababu ya kuumiza akili kufikiria uchaguzi, hizi siasa zina mambo mengi, muda mwingine watu wanajichagua tu,” alisema.
Kwa mujibu wa mwanachama huyo, umefika wakati amekata tamaa hasa ukizingatia kuna malalamiko ya rushwa.
Hoja kama hiyo iliibuliwa na mwanachama mwingine, Hugo Kimaryo aliyesema ni mbinu inayotumika na wagombea kushinikiza ushindi.
Ingawa inatumika kama mbinu, alieleza ni wajibu wa mamlaka kufuatilia na kuhakikisha inaidhibiti.
“Siwezi kupinga rushwa kutotumika kwa sababu wagombea huwa na njia tofauti, lakini Chadema kama taasisi kubwa hata mamluki hawakosi kukichezea, ila katiba ipo inaelekeza kila kitu ikiwamo uchaguzi na mambo ya rushwa” alisema Kimaryo.
Madai ya kuwepo makundi
Hata hivyo, kumekuwa na madai ya Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), kumuunga mkono Joseph Mbilinyi katika kinyang’anyiro ya uenyekiti wa kanda ya Nyasa, huku wanawake (Bawacha) wakihusishwa na Peter Msigwa.
Mwenyekiti wa Bavicha mkoani Mbeya, Elisha Chonya alilipinga hilo, akisema hawakuwahi kukaa kikao kulijadili hilo na kwamba kila mmoja anampenda mgombea wake kwa utashi wake.
“Mimi mwenyekiti wa Bavicha sijawahi kukaa na vijana tukakubaliana kumuunga mkono mgombea fulani, vivyo hivyo kwa Bavicha sidhani kama wanaye mtu wao, bali yale ni mepenzi ya mtu binafsi,” alisema.
Alisema alishawahi kupinga madai kuwa anamuunga mkono Sugu kwa kuwa hana upande aliouchagua, ingawa aliwabariki waliokwenda kuwachukulia fomu wagombea wote.
Mwenyekiti wa Bawacha mkoani humo, Elizabeth Mwakimomo naye alikanusha uvumi huo, akisema hata walioonekana kwenda kumchukulia fomu, haikuwa kwa niaba ya baraza hilo.
“Wale walitoka kwenye Bawacha, lakini haikuwa kwamba wametumwa, kila mmoja na mapenzi yake ndio maana mimi Mwenyekiti namuunga mkono Sugu” alisema Elizabeth.
Mkoani Iringa nako, Katibu wa Bavicha wa Mkoa huo, Necto Kitiga alisema kila mmoja anao upande wake kutokana na historia ya wagombea na kwamba alimpa nafasi kubwa zaidi Msigwa.
“Kila mmoja anamuamini mtu wake kutokana na namna anavyoona anafaa, siyo rushwa bali mapenzi ya mtu, kila mgombea anayo nguvu yake, lakini namuona anayetetea kuweza kushinda” alisema Kitiga.
Kanda ya Victoria
Katika kanda ya Victoria iayojumuisha mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera, wanaotarajia kuchuana na Mwenyekiti mstaafu wa Kanda hiyo Ezekiel Wenje na John Pambalu
Mfuasi wa chama hicho Hamisa Ramadhani aliliambia gazeti hili kuwa mvutano wa uongozi kati ya Wenje na Pambalu ni jambo lililotarajiwa kutokana na kukubalika kwa kila mmoja.
“Siku Wenje anachukuliwa fomu nilikuwepo kushuhudia na nyimbo tukaimba lakini siku Pambalu kafuata fomu pia nilikuwepo kumshangilia. Kwa ufupi wote wana kitu ndani yao. Maamuzi tunawaachia wanaohusika kutangaza nani ni nani,” alisema.
Paulo Mzenga mwanachama wa Chadema mkoani Mwanza, alieleza kusikitishwa na madai ya rushwa katika uchaguzi huo, akisema inahatarisha uhali wa chama hicho.
"Mimi naona chama kimeingiliwa na nguvu ya nje, watu wanatumia sana fedha katika kupata kura na kwa mwenendo huu tukiendelea tutapotea kabisa kwa sababu ukianza kuona wapiga kura wanapewa fedha hiyo ni ishara ya rushwa na kwa Mkoa wa Mwanza ndo usiseme yaani imetumika sana," alisema.
Mjumbe Kamati ya Utendaji ya Chadema Kanda ya Victoria, Sijaona Karoli aliipinga hoja hiyo akisema taarifa za madai ya rushwa ndani ya chama hicho zinasambazwa na wenye nia ovu dhidi ya chama hicho.
"Sio kweli kwamba hiyo hali ipo mimi ninavyofahamu tuavyochagua viongozi tunaangalia uwezo na sio fedha, kujituma kwake na dhamira yake hiyo dhana ya kusema kuna rushwa inajengwa na washindani wetu kwa lengo la kutuharibia," alisema.
Wanazuoni
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Aviti Mushi alisema kamati kuu hiyo itakuwa ya aina yake kulingana na yanayondelea hasa kauli ya Lissu iliyoibua mjadala ndani na nje ya Chadema.
"Kamati kuu ndio chombo kikubwa pia ndani ya Chadema, sasa haya mambo yanayoendelea hasa tuhuma mara sijui fedha chafu lazima wayajadili ili kuleta uhai wa chama, sambamba na matukio waliyoyafanya ili kuthamini yana mafanikio kiasi gani.
"Lissu ni mwanasheria nguli sana sidhani kama atatoa maneno asiyokuwa na uhakika nayo au ushahidi, inawezakana kauli alizozitoa zinakawa zina ukweli ndani yake na kamati kuu ijadili na kuzingatia maelezo yake kama ni uchunguzi ufanyike basi," alisema Dk Mushi.
Dk Mushi alizungumzia suala la uchaguzi wa kanda, akisema ni utaratibu mzuri uliowekwa na Chadema wa kuwahoji wagombea wao waliojitokeza kuwania nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.
"Ni jambo zuri kuwafanyia usahili wagombea inawezekana wengine walijaza fomu kwa kujaribu, lazima mgombea atambue anajuaye nafasi anayoitaka na kwa nini anaona anafaa kuchaguliwa au maendeleo gani atakayoyaleta katika nafasi hiyo," alisema Dk Mushi. |
Mwezi mmoja baada ya Serikali kubaini jokofu la nyumbani likitumiwa kuhifadhia damu mkoani Shinyanga | Mwezi mmoja baada ya Serikali kubaini jokofu la nyumbani likitumiwa kuhifadhia damu mkoani Shinyanga, jambo kama hilo limetokea katika Hospitali ya Magunga wilayani Korogwe katika Mkoa wa Tanga.
Kutokana na vitendo hivyo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Dk Festo Dugange ametangaza kuchukua hatua dhidi ya waliohusika.
Kabla ya tukio la Magunga mkoani Tanga, Tamisemi ilibaini ukiukwaji wa manunuzi ya majokofu ya kuhifadhia damu katika Kituo cha Afya cha Mwalugulu katika Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga.
Hilo lilibainika Aprili mwaka huu, katika ziara ya usimamizi shirikishi iliyofanywa na Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Tamisemi na mwezi mmoja baadaye katika ziara hiyo hiyo mkoani Tanga likabainika lingine.
lilivyotokea
Taarifa ya Tamisemi iliyotolewa jana, inaeleza Mkurugenzi wa huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa wizara hiyo, Dk Rashid Mfaume alibaini jokofu la matumizi ya nyumbani likitumika kuhifadhia damu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tukio hilo lilitokea katika Hospitali ya halmashauri ya mji Korogwe Magunga.
Kutokana na tukio hilo, Dk Mfaume alionyesha kukerwa huku akielekeza kufanyika utaratibu wa haraka wa upatikanaji ya jokofu maalumu la kuhifadia damu.
"Hili jokofu mnalotunzia damu ni kama tulilolikuta kule na hii tumeletewa na mdau. Tumetoka Shinyanga Mwalugulu tumewasema tukajua huku, tukidhani mmejifunza,” alisema.
“Mji wa Korogwe mna wataalamu wa kununua majokofu mazuri ya kuyahifadhi maabara tumeenda tumekuta majokofu sita jumla," alisema.
Kauli ya Waziri
Kutokana na hayo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) anayeshughulikia masuala ya afya, Dk Festo Dugange alisema kitendo kilichofanyika ni ukiukwaji wa sera, kanuni na sheria za afya.
Sheria hizo, alisema zinaweka wazi aina ya jokofu linalopaswa kutumika katika kila kazi ya hospitali, kituo vya afya na hata zahanati.
Kitendo cha kutumia jokofu lisilostahili kuhifadhia damu, kwa mujibu wa Dk Dugange ni ukiukwaji wa kanuni na sheria hizo unaofanywa kwa makusudi na baadhi ya watumishi katika halmashauri.
Naibu waziri huyo alisisitiza kutumika kwa majokofu hayo hakumaanishi kwamba yanayostahili hayapo, isipokuwa ni makosa ya watumishi wa sekta ya afya katika maeneo husika.
“Shida sio kwamba vifaa havipatikani shida ni baadhi yao wameamua kukiuka taratibu za kisheria,” alisema.
Kwa kitendo cha watumishi hao, Dk Dugange alisema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao, huku wengine wanaofanya hivyo wakisakwa ili waadhibiwe.
Mtazamo wa kitaalamu
Mtaalamu wa damu salama, Ndeonasia Towo alisema uhifadhi wa damu unahitaji jokofu lenye uwezo wa kutoa nyuzijoto kuanzia mbili hadi nane.
Pamoja na kutoa nyuzijoto hizo, Towo alisema jokofu hilo lazima liwe na mlango wa kioo utakaowezesha kuziona damu zilipohifadhiwa bila kulazimika kufungua kila muda.
Kwa mujibu wa Towo aliyewahi kuwa Ofisa Tawala Damu Salama Kanda ya Mashariki, hata jokofu la nyumbani linaweza kutumika iwapo litakuwa na vifaa saidizi.
Vifaa hivyo, alisema ni kile kitakachopima joto linalozalishwa na jokofu husika na kuhakikisha halipungui nyuzijoto mbili na halizidi nane.
“Lakini lazima pia liwe na kioo. Lakini kama hakuna kioo na hakuna kifaa maalum cha kujua nyuzijoto zinazozalishwa hilo jokofu halitafaa kuhifadhia damu,” alisema.
Kinyume na kuhifadhi katika mazingira hayo, alisema damu itapunguza ubora wake na kusababisha isidumu muda mrefu.
Alisema damu iliyohifadhiwa kwa kuzingatia vigezo hivyo, aghalabu hudumu kwa siku 35.
Hata hivyo, Ofisa mhamasishaji wa damu salama Kanda ya Kati, Bernadino Medaa aliwahi kuiambia Mwananchi kuwa, kuhifadhi damu kinyume na utaratibu huo kunauwa seli hai na haifai kutumika.
“Ni bora kutumia (majokofu) ya kitabibu kwa sababu ya ule ubora wa kuhifadhi damu yenyewe, yale ya nyumbani ni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, unaweza ukaweka maji, nyama, mboga; lakini damu yenyewe ina utaratibu wake tangu inapochukuliwa kwa mtu,” alisisitiza.
Kwa mujibu wa Medaa, majokofu ya damu huwa na vyumba vinavyowezesha kuwa na mpangilio mzuri, tofauti na majokofu y matumizi ya nyumbani.
Alisema inashauriwa damu zikae kwenye jokofu maalumu zilizoainishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) au wataalamu wa afya kwenye nchi husika ili damu isiharibike, ikienda kwa mgonjwa iende kumsaidia.
Alisema damu ikiganda hairuhusiwi kwenda kwa mgonjwa. |
Huenda bei ya gesi ya kupikia ikapungua kutoka ile inayouzwa sasa, baada ya Serikali kuanza utekelez | Huenda bei ya gesi ya kupikia ikapungua kutoka ile inayouzwa sasa, baada ya Serikali kuanza utekelezaji wa mkakati wa matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Dalili ya kupungua bei ya nishati hiyo, imetokana na kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuitaka Wizara ya Nishati ishirikiane na sekta binafsi kuona namna ya kuifanya bei ya gesi iwe himilivu.
Pamoja na hatua hiyo itakayoshinikiza matumizi ya nishati safi, mkuu huyo wa nchi ametoa marufuku ya matumizi ya kuni na mkaa kupikia kwa taasisi za umma na binafsi zinazohudumia watu zaidi ya 100.
Hatua hizo zote zinalenga kuweka msisitizo wa utekelezaji wa mkakati wa matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, unaotaka kufikia mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania watumie nishati safi.
Mkakati huo unakuja katika kipindi ambacho, takwimu zinaonyesha asilimia 90 za kaya zote nchini zinatumia nishati ya kuni na mkaa. Hiyo ni sawa na kusema kati ya kaya 10, tisa zinatumia nishati isiyo safi kupikia.
Hali hiyo inatajwa kusababisha athari zikiwemo za magonjwa ya upumuaji yanayotokana na uvutaji moshi na kupoteza uhai wa takriban watu 33,000 kwa mwaka.
Hayo yalielezwa jijini Dar es Salaam jana na Rais Samia alipohutubia hafla ya uzinduzi wa mkakati wa matumizi ya nishati safi ya kupikia wa mwaka 2024/2034.
Bei ya gesi
Katika hotuba yake, mkuu huyo wa nchi aliielekea Wizara ya Nishati ikae na wadau ndani ya Serikali na sekta binafsi ili kubaini maeneo ya kufanyiwa kazi na kuongeza haraka upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa gharama himilivu.
“Kaeni na wizara muone wapi tubane, wapi tuongeze na wapi tupunguze ili tuweke bei himilivu na wananchi wengi zaidi watumie (Nishati safi)," alisema.
Dalili za kupungua kwa bei ya nishati hiyo na nyingine za kupikia pia imedhihirika katika kauli ya Rais Samia iliyotaka kuwekwa mazingira wezeshi ya upatikanaji wake, kwa kupunguza bei na kuongeza wingi madukani.
Katika msisitizo wake wa kupunguza bei ya nishati hiyo na nyingine safi za kupikia, aliibebesha Wizara ya Nishati jukumu hilo, huku Serikali kuu akisema itabeba jukumu la utoaji elimu na kutunga sera wezeshi.
“Jukumu la Serikali ni kutunga sera wezeshi kufikia malengo ya mkakati na kutoa elimu kwa wananchi, huku Wizara ya Nishati ikiwa na jukumu la kuhakikisha nishati safi inapatikana kwa uhakika na bei himilivu,” alisema.
Marufuku ya kuni, mkaa
Mkuu huyo wa nchi, alimtaka Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Dk Seleman Jafo kutangaza marufuku kwa taasisi za umma na binafsi zinazohudumia watu zaidi ya 100, kutumia kuni na mkaa kupikia.
Rais Samia alimtaka waziri huyo kuhakikisha katazo hilo linaanza Agosti mwaka huu, akilenga kile alichoeleza, kuzishinikiza taasisi hizo zihamie kwenye matumizi ya nishati safi.
Hata hivyo, marufuku ya Rais Samia inakuja katika kipindi ambacho kati ya magereza 126 zilizopo nchini, 76 zinatumia nishati safi ya kupikia.
Sambamba na magereza, kati ya vyuo vya elimu 35 vilivyopo 30 zinatumia nishati safi kwa ajili ya kupikia, kwa mujibu wa Dk Jafo.
Kutokana na hatua iliyofikiwa na taasisi hizo, Rais Samia alisema: “(Dk Jafo) andaa katazo taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100 ni marufuku kutumia kuni na mkaa, ukipiga katazo wataingia,” alisema.
Ili kutekeleza mkakati huo, alitaka wadau wote muhimu wafikishiwe kwa njia rasmi, uwekwe kwenye tovuti ya wizara ya nishati na utafsiriwe kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.
Mfuko wa nishati safi
Rais Samia alitaka kutungwa sheria itakayounda mfuko wa kuendeleza nishati safi ya kupikia kufikia mwaka 2025, akisisitiza Serikali itatafuta namna ya kuujazia.
Katika kuujaza mfuko huo, aliahidi kuendelea kutumia majukwaa mbalimbali ya kimataifa ili kuzishawishi nchi zilizoendelea zitekeleze ahadi ya kutoa fedha kwa nchi zinazoendelea kwa ajili ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Alieleza fedha hizo zitakazotolewa, pamoja na mambo mengine zitatumika katika utekelezaji wa mkakati huo.
Katika hotuba yake hiyo, alitaka wakuu wa Mikoa waongezewe kipengele cha matumizi ya nishati safi kama mmoja ya vigezo vya kupima utendaji wao.
Lakini aliwataka wakuu wa mikoa kuwafikia wadau na kuwatambua ili wafikishe nishati hizo katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa.
Kwa mujibu wa Rais Samia, kuna haja ya nishati safi kuingizwa katika dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2050, huku Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikitakiwa kujipanga ili kutekeleza majukumu yake yaliyopo katika mkakati huo.
Katika hotuba yake hiyo, alimpongeza January Makamba, akisema alipokuwa Waziri wa Nishati ndiye aliyekuja na ajenda hiyo kwa kasi.
Kwa mujibu wa Rais Samia hekta 469,000 za misitu zinakatwa kila mwaka na nishati za kuni na mkaa ni moja ya chanzo kikuu cha hayo.
Kwa kadri misitu inavyopotea, alisema utafika wakati hata upatikanaji wa nishati ya kuni na mkaa utakuwa mgumu na hivyo kuwafanya wananchi watumie muda mwingi kutafuta nishati kuliko chakula.
“Yaani kutafuta chakula ni rahisi kuliko kwenda kutafuta chakula chenyewe,” alisema.
Katika utekelezaji wa nishati safi ya kupikia, alitaka sekta binafsi ije na mbinu kuleta teknolojia rahisi ya matumizi ya nishati akitolea mfano wa kulipia kwa kadri utakavyotumia.
Akizungumzia mkakati huo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alisema kazi ya maandalizi yake ilitekelezwa na kamati ya kitaifa inayojumuisha wizara, idara, wakala na wataalamu kutoka taasisi za elimu, washirika wa maendeleo, asasi za kiraia na sekta binafsi.
Alisema uundaji wa kamati hiyo ulizingatia kuhakikisha ushiriki wa wadau wote muhimu katika utayarishaji wake wanashirikishwa.
Kwa mujibu wa Majaliwa, kamati hiyo pia inajumuisha pande mbili za muungano yaani Bara na Zanzibar.
Majaliwa alisema mkakati huo umezingatia masuala ya kisera, miongozo na kanuni zinazosimamia utendaji yatakayosaidia kupunguza matumizi ya nishati ya kuni na mkaa.
Mambo mengine alisema ni kuondoa vikwazo vya uendelezaji nishati safi ya kupikia na uratibu wa namna bora ya kushirikisha wadau katika mnyororo wa thamani wa nishati safi ya kupikia.
Alieleza mkakati huo dhima yake ni kuhakikisha upatikanaji wa nishati safi na nafuu
Alisema wanaoanisha sera, sheria, kanuni na miongozo ili iwe wezeshi kwa wote wanaoanza kutoa huduma ya nishati safi ili iwe rahisi kwa kila mmoja kuipata.
Dira yake ni kila mtanzania atumie nishati safi ya kupikia ili kulinda afya zao.
Kwa mujibu wa Majaliwa, mkakati huo utagharimu Sh4.6 trilioni na kwamba utekelezwaji wake utahusisha wadau wote.
Kwa upande wa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko alisema atahakikisha mkakati unaozinduliwa hauishii kuonekana kwa kupigwa picha, badala yake unazaa matunda tarajiwa.
Wadau
Ili kurahisisha upatikanaji wa nishati safi na kuwezesha bei himilivu, Meneja wa Masoko wa Kampuni ya Gesi ya Oryx, Peter Ndomba alisema ni muhimu kuondoa kodi katika jiko na viungnishi vyake.
“Katika kukaa kwetu na Serikali tutaanzia hapo kwa sababu majiko haya yatashuka bei na watu wote watamudu gharama,” alisema.
Pamoja na hilo, alisema Serikali inapaswa kutoa ruzuku kwenye gesi ili kurahisisha kama inavyofanywa katika baadhi ya mataifa.
Mkazi wa Same mkoani Kilimanjaro, Stella Mramba alisema mkakati huo umekuja wakati mwafaka kwa kuwa wananchi wanahitaji matumizi ya kuni lakini hazipatikani kutokana na uchache wa misitu na ongezeko la watu.
"Tunaishukuru Serikali tunapata shida sana na matumizi ya kuni ambazo hivi sasa kuzipata ni nadra katika eneo tunaloishi,lakini wakati huohuo tunaambiwa tulinde mazingira.Sasa uamuzi huu tunaona mabadiliko makubwa katika safari ya wananchi kutumia nishati safi ya kupikia," alisema. |
Hivi unajua barabara inapowekwa kiraka, kinapaswa kidumu kwa saa 72 tu, kisha kiondolewe na ufanyik | Hivi unajua barabara inapowekwa kiraka, kinapaswa kidumu kwa saa 72 tu, kisha kiondolewe na ufanyike ukarabati?
Si hivyo tu, hata barabara inapokatwa kwa ajili ya kuwekwa kiraka, utekelezwaji wake unapaswa kufanyika kwa muda usiozidi saa 48.
Kwa mujibu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), uwekaji wa kiraka ni mbinu ya dharura inayofanywa kutoa mwanya kwa barabara iliyoathiriwa na mshimo iendelee kutumika.
Licha ya matakwa hayo ya kitaalamu, watumiaji wa barabara nchini wanaeleza uhalisia tofauti, wakifafanua viraka vingi vinavyowekwa kwenye barabara hudumu kwa zaidi ya saa hizo.
Si viraka pekee, wanasema katika baadhi ya barabara hasa zenye mashimo hukatwa kwa ajili ya kuwekwa viraka, lakini inachukua muda mrefu bila hilo kutekelezwa.
Hali hiyo kwa mujibu wa watumiaji hao, inasababisha ajali, msongamano na wakati mwingine huongeza gharama za uendeshaji biashara ya usafiri wa barabarani.
Hata hivyo, kuchelewa kwa ukarabati wa barabara baada ya kiraka, aghalabu husababishwa na mvua kama inavyofafanuliwa na Mkuu wa Idara ya Mipango wa Tanroads Dar es Salaam, Mhandisi Clever Akilimali.
Mazingira kama hayo, Machi 2015, katika eneo la Changalawe Mafinga, Mkoa wa Iringa yalisababisha ajali kati ya lori la mizigo la kampuni ya Cipex na basi kampuni ya Majinjah Express lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam kugongana.
Ajali hiyo ilisababisha vifo vya watu 42 na wengine 23 kujeruhiwa.
Nyasio Pascal aliyekuwa shuhuda wa ajali hiyo alisema aliliona lori hilo likijaribu kukwepa mashimo kwenye barabara hiyo ambayo ni nyembamba na mara likaanza kuyumba kulia na kushoto baada ya kuykanyaga shiko ndipo lilipofuata basi na kugongana nalo.
Uhalisia barabarani
Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, madereva bodaboda jijini Mbeya wametaja barabara za Mataa kwenda Uwanja wa ndege wa zamani kata ya Pambogo, Kabwe kwenda Isanga na Isyesye hadi Itiha kuwa miongoni mwa zile zenye viraka na mashimo ya muda mrefu.
Francis Joel ni miongoni mwa madereva hao, alisema matokeo ya hali hiyo ni kuwepo kwa ajali nyingi katika barabara hizo.
Sambamba na ajali, madhira mengine ya barabara hizo, alisema huharibu vyombo vya usafiri na na kuweka mashakani usalama wa madereva.
"Hata kabla ya mvua barabara nyingi za Jiji la Mbeya sio rafiki kabisa zimekuwa zikiweka rehani maisha yetu licha ya kulipia ushuru lakini bado Serikali haitambui mchango wetu," alisema Joel.
Kwa upande wa Mussa Nassoro anayeendesha balaji mkoani humo, anaitaja barabara inayotoka Magereza kwenda Hospatali ya Rufaa, yenye hali mbaya licha ya matengenezo ya mara kwa mara inayofanyiwa.
Katika Mkoa wa Arusha nako, Amina Bakari alisema mashimo ndiyo changamoto kjbwa katika barabara za eneo hilo na hivyo kuchelewesha watoto wanapokwenda shule.
Rukia William naye pamoja na mashimo na viraka, kukosekana kwa vivuko ni changamoto nyingine katika barabara za Arusha.
Katika maelezo yake aliitokea mfano barabara ya Serengeti iliyoharibika na kusababisha baadhi ya biashara zifungwe na hivyo kuatjiri mapato ya Serikali.
Vyombo vya usafiri vya watumiaji wa barabara ya Kenyatta mkoani Mwanza, vinaharibika mara kwa mara kutokana na kile walichosema, barabara ina viraka vingi.
Barabara hiyo ina zaidi ya kilomita 22 inayoanzia mjini kati kuelekea hospitali ya Wilaya ya Nyamagana (Butimba), stendi ya mabasi Nyegezi, Buhongwa kisha Nyashishi.
Dereva wa daladala, Dickson Mwitta alisema barabara zenye viraka zina haribu magari kwa asilimia 100.
“Lami inapokuwa hivyo (viraka) usababisha dereva kutumia muda mwingi awapo safari maana utembea kwa tahadhari kubwa ili kulinda chombo chake kisipate madhara na kulinda watumiaji wengine pia. Barabara za mjini kuwa mbovu kwanza ni taswira mbovu ya halmashauri yetu,” alisema Mwitta.
Dereva bodaboda Fikiri Thobias alishauri kuliko Serikali kuweka taa za barabarani hata sehemu zisizo za lazima ni bora zingefumua barabara zenye viraka, kuleta ahueni kwa watumiaji.
Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Mwenyekiti wa bajaji wilayani humo, Moses Miyo alieleza ubovu wa barabara unasababisha kuharibika mara kwa mara kwa vyombo vyao vya usafiri.
"Changamoto ya ubovu wa miundombinu ni kubwa kwa sababu barabara ikiwa mbovu hatuwezi kupata faida hata mmiliki baada ya kupata faida anapata hasara kwa ajili muda mwingi unakuwa unatengeneza vyombo hivyo," alisema Miyo.
Salum Abdallah, aliyekuwa akisafiri kwa gari ndogo kutoka Dodoma kwenda jijini Dar es Salaam alisema baadhi ya viraka barabarani vinapaswa kutengenezwa haraka ili kunusuru na ajali.
“Kuna muda nilikwepa bonde lililochongwa, mbele kukawa na gari inakuja, ni Mungu tu alisaidia kuwahi kurudi kwenye mstari uelekeo, lakini ni changamoto sana,” alisema.
“Kama viraka vinawekwa basi vitengenezwa haraka, kuviacha vilivyo ni hatari sana. Kuna ile ajali ilitokea Iringa miaka ya nyuma na kuua zaidi ya watu 40, chanzo ilikuwa mashimo. Kwa hiyo Serikali inapaswa kutengeneza barabara zake haraka,” alisema.
Lakini, Mussa Saidi aliyesafiri kwa gari ndogo kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma naye alieleza uwepo wa mashimo na viraka vingi kwenye barabara.
Alisema ukiachana na kuongeza muda wa safari, hali hiyo inahatarisha usalama kwa kuwa barabara hazijatulia.
"Kuna wakati inabidi muanze kukwepa mashimo, unaona kabisa dereva anavyohangaika karibu atoke barabarani ni hatari sana," alisema.
Mabasi
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Mabasi (Uwamata), Majura Kafumu anasema mbali na kuendesha kwa tahadhari kama wasafirishaji wa abiria pia aliwataka wananchi kutoa ushirikiano wa kuweka alama za hatari pindi wanapoona eneo la barabara si salama.
Hiyo ni kutokana na kile alichokieleza kuwa, wakati mwingine uharibifu katika barabara huweza kutokea ndani ya muda mfupi tangu dereva kutua njia hiyo hivyo ni muhimu ushirikiano wa karibu ukatolewa na wananchi.
“Ikiwa wananchi wana mashaka na eneo Fulani basi waweke alama ili kuonyesha usalama ukoje katika eneo husika ili kuwasaidia madereva, wakati mwingine sisi tunaendesha ila hatujui hali halisi ikoje huko chini, unaweza kuona ni ufa mdogo kumbe ni hatari,” amesema Kafumu.
Wakati yeye akiyasema hayo, mmoja wa wamiliki wa daladala jijini Dar es Salaam, Ghalib Mohammed amesema ubovu wa miundombinu ya barabara umekuwa ukisababisha kuharibika kwa magari jambo linaloongeza gharama za uendeshaji.
“Gharama za uendeshaji zinakuwa za hali ya juu, ajali nyingi kwa madereva pia inaleta usumbufu kwa watumiaji wa barabara kutokana na foleni,” amesema Mohammed.
Wakati yeye akiyasema hayo, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, Salum Pazzy kutoka Mamlaka ya udhibiti wa Usafiri Ardhini amesema kama wasimamizi wamekuwa wakihakikisha wanaratibu usalama ardhini.
“Kama kuna shida ya miundombinu tnawaita wadau na kuwaambia hivyo tumekuwa tunaratibu kwa namna hiyo kwa sababu suala la ujenzi liko chini ya Wizara ya Ujenzi,” amesema Pazzy.
Ukongwe wa barabara tatizo
Umri wa barabara ni moja ya sababu inayofanya mamlaka zilazimike kuweka viraka vingi, kama inavyoelezwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura), Victor Seif.
“Umri unaweza kuwa umefikia lakini rasilimali za kufanya maboresho zinakuwa hazitoshi,” alisema Seif.
Katika ufafanuzi wake, alisema kitaalamu baada ya barabara kukatwa, kiraka kinapaswa kuwekwa ndani ya saa 48.
Lakini utekelezaji wa hilo, alisema unakwamishwa na changamoto ya upatikanaji wa lami kwa wakati kwa ajili ya kuziba mashimo.
“Kwa sasa tumepiga marufuku, wanapokata barabara wahakikishe inazibwa kwa wakati na tumekuwa tukifuatilia hili,” alisema Seif.
Alisema ni mbaya zaidi katika mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma na kwamba, barabafa nyingi zinatakiwa kufanyiwa matengenezo.
Hoja ya ukongwe wa barabara inazungunzwa pia na Meneja wa Tanroads mkoani Mwanza, Pascal Ambrose aliyesema baadhi ya miundombinu hiyo ina muda mrefu.
“Mfano barabara ya kwenda Shinyanga na Musoma kutokea Mwanza ni za muda mrefu kwa hiyo matabaka yake ya chini yamechoka sasa maji yakiingia yanafumua na kusababisha viraka kuwa vingi hali inayopelekea kuathiri usafirishaji ikiwa ni pamoja na vyombo vya moto kuharibika,” alisema.
Alieleza viraka huwekwa kuondoa changamoto kubwa inayokuwepo, hata hivyo ni vigumu palipowekwa kiraka kufanana na pasipowekwa.
Kuhusu barabara ya Kenyatta, Ambrose alisema wana mpango wa kuifumua na kuijenga upya kwa njia nne na tayari upembuzi yakinifu ulishafanyika kinachosubiriwa ni fedha kutoka serikalini.
Tanroads
Akizungumzia suala hilo, Mkuu wa Idara ya Mipango wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Clever Akilimali amesema kwa kawaida kipande cha barabara kinapokatwa kinapaswa kuzibwa ndani ya saa 72 lakini wakati mwingine mvua imekuwa kikwazo.
Hiyo ni kufuatia kile alichokieleza, ili matokeo tarajiwa kupatikana katika uwekaji wa viraka barabara inapaswa kuwa kavu.
“Sasa hii mvua ndiyo inaleta changamoto, hauwezi kupika lami na kwenda kuziba sehemu ambayo imeloana, inataka sehemu ambayo ni kavu, ndiyo maana wakati mwingine tunatumia zege kuziba kwa muda au kuweka vipande vya lami tulivyokata sehemu nyingine katika shimo husika,” amesema Akilimalio.
Kanuni nyingine ili kupata matokeo tarajiwa, joto ambalo linakuwapo katika uji wa lami uliopikwa linatakiwa kuwa katika kiwango kilekile hadi linapofika eneo la ujenzi.
“Hatupendi kuacha hali ilivyo, ndiyo maana mtu akikata eneo la barabara anatakiwa kuziba siku hiyohiyo kama si lami uzibe na zege,” amesema Akilimali.
Akizungumzia viraka katika barabara amesema wakati mwingine umri wa barabara unaweza kuwa umepitwa na wakati lakini inafanyiwa maboresho kwa kutumia mfumo huo wakati wakisubiri fedha zilizoombwa ili ifanyiwe kazi.
“Mahitaji ni makubwa, sasa unakuta wakati mwingine umri wa barabara ni miaka 15 ila ina miaka 25, tunajitahidi kuziba ili kuiweka katika hali ya usalama. |
Safari ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Chama cha ACT Wazalendo imefikia leo, huku viongozi wake wak | Safari ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Chama cha ACT Wazalendo imefikia leo, huku viongozi wake wakitabiri taswira ya chama hicho katika miaka 10 ijayo.
Kwa mtazamo wa viongozi hao, katika miaka 10 ijayo, chama hicho ndicho kitakachoshika hatamu ya uongozi serikalini, kielelezo cha ushirikishwaji wa vijana katika siasa na taswira halisi ya siasa za upinzani.
Hata hivyo, mtazamo huo wa viongozi unashabihiana na maoni ya wanazuoni kuhusu chama hicho katika miaka 10 ijayo, wanaosema kilivyokuwa kwa kasi ni dhahiri kitaleta mageuzi katika siasa za Tanzania.
Chama hicho kilianzishwa Mei 5, 2014 chini ya uenyekiti wa Anna Mghwira, ambaye Machi 4, 2021 alihamia CCM ikiwa ni miaka mitatu tangu alipoteuliwa na Hayati John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Mghwira aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa miaka miwili baada ya kuwa miongoni mwa wagombea wa Urais wa Tanzania, akipeperusha bendera ya chama cha ACT Wazalendo na baadaye Julai 22, 2021 alifariki dunia.
Akizungumza na Mwananchi, Kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu alisema katika miaka 10 ijayo itakuwa safari ya kukiona chama hicho kikiendelea kuaminiwa.
Msingi wa kuaminiwa kwake ni kile alichoeleza, katika miaka 10 iliyopita kilijipambanua kuwa sauti ya wananchi.
Kwa mtazamo wa Dorothy, ndani ya miaka 10 hiyo ACT Wazalendo itashika hatamu za juu za uongozi kwa kupigiwa kura na wananchi wengi.
"Haitwakuwa wenyeviti wa Serikali za Mitaa pekee, bali Madiwani, Wabunge na hata nafasi za juu zaidi ikiwemo ya Urais kwa pande zote za muungano," alisema.
Hata hivyo, alisema katika kipindi hicho Watanzania watashuhudia mabadiliko makubwa ya kitaasisi, bunge na serikalini.
Hata hivyo, alieleza kiu kubwa ya chama hicho baada ya kujenga msingi kwa miaka 10 ni ushindi wa kushika nafasi mbalimbali ndani ya Serikali
Watafikaje huko?
Siri ya mafanikio hayo ni kile alichodai uwepo wa utaratibu wa kujitathmini na hilo lilianza kufanyika tangu baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.
Baada ya uchaguzi huo, Kiongozi huyo alisema waliangalia maeneo waliyofanya vibaya kwa ajili ya kuyaboresha na kuweka mkakati wa muda mrefu.
"Tumekuwa na mkakati uliotutoa 2020 kuelekea mwaka 2025 na kama sehemu ya mikakati wetu matokeo yameonekana katika mkutano mkuu wetu uliofanyika mwaka huu," alisema.
Katika mkutano huo, alisema wajumbe kutoka majimbo yote ya uchaguzi nchini walifika, ukilinganisha na mwaka 2020 ambapo asilimia 70 tu ndiyo walihudhuria.
Alieleza hicho ni kielelezo cha kuwa na uwakilishi wa wanachama katika kila ngazi.
Kinavyojitifautisha na vyama vingine
Utofauti wa ACT Wazalendo na vyama vingine vya siasa ni uzoefu wa waasisi wake, walioupata kutoka katika vyama mbalimbali vya siasa nchini.
Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, Issihaka Mchinjita ACT Wazalendo ilipoanzishwa wanachama wengi kutoka Chadema na CUF walijiunga nacho na kimsingi wanajua nini kosa na nini sahihi katika uendeshaji wa vyama.
"Hawa wanachama walikuwa na uzoefu wa yale mazuri ya Chadema na mabaya yake, lakini walikuwepo waliokuwa na uzoefu wa madhaifu ya CUF na mazuri yake," alisema.
Kwa sababu hiyo, alisema ndiyo maana Chama hicho kimejikita katika kujenga mfumo imara wa uongozi wa ndani.
Alieleza chama hicho kina mfumo mzuri wa kutengeneza, kuzalisha na kubadilisha viongozi kutoka ngazi na awamu moja kwenda nyingine.
"Tunahamu kiongozi wetu wa chama alikuwa Zitto Kabwe na sasa ameondoka amemwachia Dorothy Semu. Kwa hiyo ule mfumo wa kubadilisha viongozi wake kwa kuangalia Hali hitajika kwa wakati husika ni Bora kuliko vyama vingine," alisema.
Mabadiliko mfumo wa siasa
Alisema ACT Wazalendo ndicho chama kilichoasisi mwenendo wa siasa za upinzani kutoka kukosoa pekee hadi kukosoa na kuja na sera mbadala.
"Mara nyingi siasa za upinzani zilikuwa ni kukosoa Serikali tu bila kupendekeza sera mbadala ambayo vyama vingi ukiondoa CCM hawana," alieleza.
Mzizi wa hilo, alisema ni utafiti ambao aghalabu chama hicho kimekuwa kikiufanya kabla ya kuamua kufanya jambo lolote.
Imani kwa vijana
Naibu Mwenezi wa chama hicho, Shangwe Ayo alisema imani kwa vijana ndicho kinachokifanya chama hicho kuwa kimbilio lao.
Kielelezo cha hilo, alisema ni historia yake ndani ya chama hicho, akisema alijiunga mwaka mmoja uliopita lakini ameaminiwa na kupewa nafasi ya uongozi wa kitaifa.
"Kwa kawaida vijana wengi wananyimwa nafasi katika vyama vingine lakini falsafa ya ACT Wazalendo ni mwanachama aliyeingia leo na yule wa miaka 10 iliyopita wote wana haki na nafasi sawa," alisema.
Alieleza utaratibu huo wa chama hicho, unafanya vijana wengi kuwa na kiu ya kujiunga nacho wakiamini watapata nafasi ya kuonyesha uwezo wao wa uongozi.
Mtazamo wa wasomi
Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Matrona Kabyemela alisema kuna taswira ya ACT Wazalendo kukua zaidi baada ya miaka 10 ijayo.
Alisema mara nyingi vinapoanzishwa vyama vya siasa, watu hutarajia vitakufa, lakini ACT Wazalendo imejitofautisha na vingine katika hilo.
“Kama tunavyojua kwa sasa ndiyo chama kikuu cha upinzani kwa upande wa Zanzibar na kipo ndani ya Serikali kwa sasa. Kwa upande wa bara bado lakini kinaonyesha nguvu kubwa,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk Kabyemela, hatua ya kuendana na siasa za wakati ni jambo lingine linalodumisha uhai wa chama hicho, akifafanua kimewekeza kwa vijana wenye taaluma na kinawatumia ipasavyo.
Maandalizi ya maadhimisho
Chama hicho kinatarajiwa kufanya maadhimisho ya kuzaliwa kwake katika kila mkoa nchini kupitia shughuli mbalimbali.
Mkoa wa Kigoma ndiko kilele cha maadhimisho ya sherehe hizo kinakofanyika leo kwa shughuli mbalimbali.
Miongoni mwa shughuli hizo ni kutembelea vituo vya kulea watoto yatima kutoa misaada na kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya umma.
Kuelekea maadhimisho hayo, wafuasi wa chama hicho wamekusanyika katika Ofisi ya ACT Wazalendo mkoani humo kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa hadhara unaofanyika leo.
Bendera za chama hicho zimepandishwa na nembo mpya imezinduliwa, ikiwa ni ishara ya ACT Wazalendo kujihuisha. |
Baada ya mfululizo wa mvua za El-Nino kwa takriban miezi saba, baadhi ya mikoa nchini inatarajiwa ku | Baada ya mfululizo wa mvua za El-Nino kwa takriban miezi saba, baadhi ya mikoa nchini inatarajiwa kukumbwa na Kimbunga Hidaya kwa siku tano mfululizo.
Iwapo hilo litatokea, hii itakuwa mara ya tatu kwa Tanzania kukumbwa na kimbunga tangu nchi ikiwa chini ya mkoloni, kama ilivyoelezwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk Ladislaus Chang’a.
Kwa mujibu wa Chang’a, kimbunga kama hicho kiliwahi kutokea mwaka 1952 mkoani Lindi, wakati huo Tanzania ikiitwa Tanganyika na kingine kilitokea miaka ya 1800.
Hata hivyo, wataalamu wanapendekeza kama nyumba zilizopo katika maeneo yatakayoathiriwa si imara, ni vema wakazi waamue kuhama kwa muda, huku wakisisitiza baadhi ya shughuli kusimama.
Taarifa kuhusu matarajio ya kimbunga hidaya, zilitolewa jana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), ikieleza kitakuwa na nguvu ya kati na umbali wa kilomita 506 Mashariki mwa Pwani ya Mtwara.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwenendo wa mfumo wa hali ya hewa baharini unaonyesha uwezekano wa kimbunga hicho kusogea karibu na Pwani ya Tanzania kuanzia usiku wa Mei 2, 2024 na kuendelea hadi Mei 6, 2024.
Uwepo wa kimbunga hicho, TMA inasema kutaathiri mifumo ya hali ya hewa na kusababisha vipindi vya mvua kubwa na upepo mkali katika mikoa kadhaa.
TMA inataja mikoa hiyo ni Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga, Morogoro, Visiwa vya Unguja na Pemba na maeneo mengine ya jirani.
Kutokana na hali hiyo, mmalaka hiyo imeshauri wa mikoa husika na wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali baharini, kuchukua tahadhari na kufuatilia taarifa za TMA.
“Pia, wanapaswa kupata ushauri na miongozo ya wataalamu wa sekta husika, ili kujikinga na athari tarajiwa,” ilieleza taarifa hiyo.
Mzizi wa kutokea kwa kimbunga hicho ni kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hewa, ambao TMA iliuripoti Mei 1, 2024.
Kama nyumba si imara ondoka
Mwanazuoni wa Chuo Kikuu Mzumbe mkoani Morogoro, Profesa William Mwegoha alisema katika hali kama hiyo yeyote mwenye makazi anayodhani si stahimilivu ni vema ahame kuepuka athari.
Kwa mujibu wa mwanazuoni huyo, kimbunga kama hicho kinachoambatana na mvua kubwa huwa hatari kwa uharibifu wa majengo.
Hatari zaidi, alisema inatokea pale nyumba iliyopo katika eneo litakaloathiriwa ama imechoka au haina uimara wa kustahimili upepo na mvua kubwa.
“Mvua inalegeza udongo, upepo unasukuma nyumba, ni vitu ambavyo vikishirikiana kama nyumba si imara dakika chache inaanguka, kwa hiyo ni vema kuondoka,” alisema.
Lakini, kama kitatokea bila mvua kubwa, Profesa Mwegoha alishauri wananchi wa maeneo yatakayoathiriwa wasitishe shughuli zao za siku zote, badala yake watulie nyumbani.
Muhimu zaidi kwa mujibu wa Profesa Mwegoha aliyebobea katika taaluma ya mazingira, ni kufuatilia taarifa za mamlaka mbalimbali ili kujua uelekeo na mwenendo wa kimbunga hicho.
“Ukifuatilia taarifa utajua wakati gani kinatarajiwa kutokea na eneo litakaloathirika zaidi na kuhakikisha maeneo hatarishi sana, watu watulie maeneo waliyopo, au kama kuondoka basi waondoke haraka,” alieleza.
Katika ufafanuzi wake, Mkurugenzi wa TMA alisema watumiaji wa bahari wanapaswa kuchukua tahadhari kwa sababu upepo mkali na mvua kubwa inatarajiwa kunyesha.
Lakini, alieleza athari pia zitarajiwe hata katika maeneo ambayo hayakubainishwa kwa kile alichofafanua kutokea kwa kimbunga huathiri mifumo ya hali ya hewa na hivyo kusababisha athari kusambaa.
“Kwa sababu kimbunga kinavyotokea unaweza kukuta ukanda wa Ziwa Victoria nao ukaathirika kutokana na mifumo ya hali ya hewa kuathiriwa,” alisema.
Hata hivyo, alisema katika hali kama hiyo TMA inafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara kwa saa 24 na itakapoonekana haja ya kutoa taarifa watafanya hivyo.
Aliwasihi wananchi kuendelea kufuatilia taarifa hizo ili kujiepusha na athari.
Pamoja na yote hayo, aliwasisitiza wananchi wasiwe na taharuki, badala yake waendelee kutekeleza maelekezo ya kitaalamu kama wanavyoshauriwa. |
Vyama vya Wafanyakazi, vimesema matumaini yao kuhusu utekelezaji wa mabadiliko ya kanuni ya kikokoto | Vyama vya Wafanyakazi, vimesema matumaini yao kuhusu utekelezaji wa mabadiliko ya kanuni ya kikokotoo na nyongeza ya mishahara yamebaki kwa Serikali.
Kauli hiyo ya wafanyakazi inakuja siku moja, baada ya Serikali kuweka wazi kuwa, tayari imesikia maoni yao kuhusu madai ya mabadiliko ya kanuni ya kikokotoo, kadhalika nyongeza ya mishaharaka.
Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango jana katika sherehe za Mei Mosi zilizofanyika jijini Arusha, alisema Serikali itaongeza mshahara hivi karibuni iwapo uchumi utaendelea kuwa stahimilivu kama ulivyo sasa.
Kwa upande wa kikokotoo, Dk mpango alisema: “Tunawategemea wataalamu wetu watushauri kuhusu suala hili la uhimilivu na uendelevu wa mifuko ya hifadhi ya jamii.
“Tunawahakikishia wafanyakazi kwamba hakuna mtu angependa kuona watu waliotumikia nchi hii wanaathirika kwa kukosa kiinua mgongo stahiki au pensheni zao,” alisema.
Kutokana na kauli hiyo ya Serikali, Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Tumaini Nyamhokya leo Alhamisi, Mei 2, 2024 ameiambia Mwananchi Digital kuwa, wanachosubiri ni utekelezaji.
Ingawa amesema anatambua mabadiliko ya mambo yote hayo hayafanyiki kwa haraka kama inavyodhaniwa na wengi, bado anaamini utekelezaji upo mikononi mwa Serikali.
Kinachompa matumaini ya kutekelezwa kwa hayo ni kile alichoeleza, Serikali imekiri kupokea mapendekezo yao na imeahidi kufanyia kazi.
“Mabadiliko mfano ya kanuni si jambo la leo na kesho, ni suala linalohusisha mchakato na unapita kwa watu wengi tukiwemo sisi kutoa maoni yetu. Lakini kwa sababu serikali imepokea tunaamini itafanyia kazi,” amesema.
Kinachompa matumaini ya kutekelezwa kwa nyongeza ya mishahara, amesema ni kuwepo kwa bodi za kima cha chini cha mishaharaka ya sekta binafsi na umma.
Amesema mara zote mishahara imekuwa ikipandishwa katika majukwaa, lakini bodi hizo ndizo zenye mamlaka ya kufanya tathmini ya kitaalamu na kuwasilisha mapendekezo yake kwa Waziri mwenye dhamana.
“Uwepo wa bodi hizi kunaleta matumaini kwamba nyongeza ya mishahara itafanywa kwa kuwa hizi ndizo zenye mamlaka ya kutathmini na kuwasilisha mapendekezo,” ameeleza.
Hata hivyo, kuhusu kikokotoo, amesema mabadiliko yaliyosababisha kupatikana kwa asilimia 33.3 kisheria yatachukua miaka mitatu kuboreshwa.
Amesema hadi sasa mabadiliko hayo yamefikia miaka miwili na kwamba umebaki mmoja ili kwa mujibu wa sheria yawe na uhalali wa kubadilishwa.
“Baada ya miaka mitatu hapo tathmini itafanyika kwa kuangalia uimara wa mifuko kisha mabadiliko ya kanuni ndiyo yataanzia hapo, tunachokifanya sasa ni kupaza sauti ili kuhakikisha mabadiliko yanafanyika wakati utakapofika,” amesema Nyamhokya. |
Matumaini ya wafanyakazi juu ya kutangaziwa nyongeza ya mishahara na mabadiliko ya kanuni ya kikokot | Matumaini ya wafanyakazi juu ya kutangaziwa nyongeza ya mishahara na mabadiliko ya kanuni ya kikokotoo cha mafao ya wastaafu katika sherehe za Mei Mosi yametoweka, baada ya Serikali kuonyesha mchakato wa utekelezwaji wa hayo unaendelea.
Nyongeza ya mishahara na mabadiliko ya kanuni ya kikokotoo ni miongoni mwa taarifa zilizotarajiwa na wafanyakazi katika sherehe hizo, lakini hakuna ufumbuzi uliotangazwa kuhusu hayo.
Katika nyongeza ya mishahara, Serikali imeahidi itatangaza hivi karibuni iwapo uchumi utaendelea kuwa stahimilivu kama ulivyo sasa.
Pamoja na ahadi hiyo ya Serikali, lakini haijaweka wazi kwamba lini itatangaza nyongeza hiyo rasmi, badala yake imesema uamuzi wa kufanya hivyo utategemea ustahimilivu wa kiuchumi.
Hata hivyo, ahadi hiyo inazua wasiwasi juu ya nyongeza hiyo, kutokana na kilichoelezwa na Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango katika sherehe hizo, kwamba kuna athari za kiuchumi zilizosababishwa na majanga ya dunia yakiwemo mafuriko.
Ni ukweli kwamba kwa takriban miezi saba, Tanzania imekumbwa na mvua za mfululizo zilizosababisha mafuriko na hivyo kuondoa uhai wa zaidi ya watu 160, huku wengine wakiachwa bila makazi.
Lakini mvua hizo hazikuishia kwa binadamu pekee, hata miundombinu ya barabara na ardhi zimeathirika, hivyo kuigharimu Serikali kuanza upya ujenzi wake.
Kwa upande wa kanuni ya kikokotoo, Serikali imesema uamuzi wa kuibadilisha utatokana na tathmini ya kina ya kisayansi ya watakwimu bima na Serikali inaamini wafanyakazi watawasilisha maoni yao.
Hayo yalielezwa jana na Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango alipohutubia sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ‘Mei Mosi’ ambazo kitaifa zilifanyika jijini Arusha.
Nyongeza mishahara
Uamuzi wa kuhuisha viwango vya mishahara, alisema unafanyika kwa kuzingatia uwezo wa kiuchumi na kibajeti, kadhalika ujuzi na utendaji wa waajiriwa.
Kuzingatiwa kwa misingi hiyo, alieleza kunalenga kuepuka kuchochea mfumuko wa bei, kuhatarisha uhimilivu wa deni la taifa na athari nyingine kwenye utulivu wa uchumi.
“Haya yote lazima yazingatiwe katika mchakato wa kuongeza mshahara na hususan katika kipindi ambacho, uchumi wa dunia umekumbwa na misukosuko mingi, ikiwemo vita vya Urusi na Ukraine, Mashariki ya kati vinavyohusisha Israel na Palestina, Lebanon, Iran na Yemen,” alisema.
Vita hivyo, alifafanua vimesababisha kuvurugika kwa mfumo wa ugavi na kupandisha bei ya mafuta, mbolea, chuma na chakula.
Si hivyo tu, Dk Mpango alisema Dunia imekumbwa na majanga mengine kama mvua kubwa na maporomoko ya ardhi yaliyosababisha uharibifu wa miundombinu, magonjwa na mafuriko.
Licha ya changamoto hizo, Dk Mpango aliweka wazi kuwa, tathmini ya Serikali, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika, zimeonyesha uchumi wa Tanzania umekuwa stahimilivu kwa kiasi cha kuridhisha.
“Hivyo, mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, Mama wa taifa, ameniagiza niwaambie wafanyakazi wa Tanzania kuwa endapo hali hii itadumu wafanyakazi wawe na matumaini kwamba atasema jambo hivi karibuni,” alisema.
Mzizi wa maelezo hayo ya Serikali kuhusu nyongeza ya mishahara ni risala iliyosomwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Henry Mkunda katika sherehe hizo, iliyoeleza umuhimu wa nyongeza ya mishahara ili wafanyakazi wamudu gharama za maisha.
Katika risala hiyo, Mkunda alisema kuna umuhimu wa kuongeza mishahara ili kutengeneza mazingira ya wafanyakazi kupata mafao makubwa watakapostaafu.
Aliijenga hoja hiyo, akieleza kutambua juhudi zilizofanywa na Serikali katika nyongeza ya mishahara mwaka jana, lakini alisema bado haikidhi mahitaji ya wafanyakazi.
“Mishahara nadhifu ina uhusiano mkubwa na upatikanaji wa mafao stahiki ya wastaafu, kwani kadri mshahara unavyokuwa mdogo na ndivyo mafao yanavyokuwa finyu,” alisema.
Mapitio ya kima cha chini ya mshahara wa sekta binafsi, makato ya kodi katika mapato yasiyo ya mishahara ni miongoni mwa mambo aliyopendekeza yafanyiwe mapitio ili kuboreshwa.
Kikokotoo
Kuhusu hoja ya kikokotoo nayo iliibuliwa na risala hiyo ya Tucta, Dk Mpango alisema uamuzi wa mabadiliko ya kanuni hiyo, utatokana na tathmini ya kina ya kisayansi ya watakwimu bima na Serikali inaamini Tucta itawasilisha maoni yake.
“Tunawategemea wataalamu wetu watushauri kuhusu suala hili la uhimilivu na uendelevu wa mifuko ya hifadhi ya jamii, tunawahakikishia wafanyakazi kwamba hakuna mtu angependa kuona watu waliotumikia nchi hii wanaathirika kwa kukosa kiinua mgongo stahiki au pensheni zao,” alisema.
Alisisitiza kupokea hoja ya mapendekezo ya Tucta kuhusu maboresho ya kanuni hiyo kwa uchambuzi zaidi, akisema Serikali ni sikivu.
Hoja iliyojengwa awali na Mkunda kuhusu kikokotoo ni wafanyakazi kutoridhishwa na kanuni mpya za kukoko0toa mafao ya wastaafu.
Katika hoja yake hiyo, alisisitiza kwa kuwa mifuko inaonyesha kuimarika Serikali ione haja ya kuboresha kanuni hizo bila kuathiri mifuko hiyo.
Wakati huo huo, Chama cha ACT Wazalendo katika taarifa yake kiliitaka Serikali kumaliza mgogoro wa Kikokotoo cha pensheni za wastaafu, kwa kurejesha kanuni za zamani za kukokotoa mafao zilizotumika kabla ya mwaka 2017.
“Zirejeshwe kanuni za zamani za kukokotoa mafao zilizotumika kabla yam waka 2017. Tunatambua kuwa hapa nchini Tanzania hali ya wafanyakazi si nzuri. Kwa kipindi kirefu wamekuwa wakipunjwa maslahi yao kutokana na sera, sheria na kanuni kandamizi zisizojali maslahi yao,” alisema Kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu.
Likizo wanaojifungua watoto njiti
Dk Mpango alisema ipo katika mchakato wa kufanyia maboresho sheria ya ajira na mahusiano kazini kwa sekta binafsi na umma ili kulinda haki za wafanyakazi wanawake wanapojifungua.
Alisema likizo ya uzazi ni miongoni mwa haki za mfanyakazi na aghalabu hutolewa kwa muda wa siku 84, iwapo mzazi amejifungua mtoto mmoja na siku 100 iwapo ni mtoto zaidi ya mmoja.
Kwa wafanyakazi watakaojifungua watoto kabla ya muda na wakalazimika kuwekwa katika chumba maalum chini ya uangalizi wa madaktari, alisema muda huo hautahesabiwa katika likizo ya uzazi.
“Iwapo mfanyakazi atajifungua mtoto au watoto njiti, kipindi cha uangalizi maalum hakitahesabiwa kama likizo ya uzazi,” alisema na kurudia akionyesha msisitizo.
Likizo ya uzazi, alieleza itaanza pale ambapo mtoto atakapomaliza kipindi cha uangalizi maalum kwa kadri madaktari watakavyojiridhisha.
Hilo litaambatana na kile alichoeleza, mzazi huyo ataruhusiwa kutoka kazini kila saa 7:30 mchana kila siku kwa muda wa miezi sita baada ya kumalizika kwa likizo ya uzazi.
Ufafanuzi huo pia, ulitokana na risala ya Tucta iliyopendekeza wazazi watakaojifungua watoto njiti wapewe likizo ya miezi sita, badala ya mitatu ya sasa.
Kitita cha bima ya afya
Katiba hotuba yake hiyo, Dk Mpango alisema baada ya malalamiko kuhusu kitita cha bima kwa wanufaika, Serikali iliunda kamati maalum ya kuyapitia na kwamba kazi hiyo inaendelea.
Wakati kazi hiyo inaendelea, alisema Serikali itahakikisha wadau wote wanashirikishwa na kutatua changamoto zilizojitokeza.
“Na kama ambavyo imeelezwa tayari Tucta imeshakutana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na ufafanuzi ulitolewa juu ya hatua zilizochukuliwa kutokana na changamoto,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk Mpango, uhai na uendelevu wa mifuko ya hifadhi ya jamii inategemea uwasilishwaji wa michango ya wafanyakazi.
Majibu haya ya Dk Mpango yalitokana na hoja iliyowasilishwa na Tucta kupitia risala yake, ikieleza umuhimu wa Serikali kuboresha kitita hicho, huku ikitaka wafanyakazi wasiathiriwe kwa makosa ya waajiri kutopeleka michango ya bima ya afya.
Katika sherehe hizo yaliibuka malalamiko ya wingi wa kodi katika mapato yasiyo ya mshahara, Dk Mpango alijibu makato yote katika mapato ya mfanyakazi kufanywa kwa mujibu wa sheria.
Katika hilo, aliwapongeza wafanyakazi kuwa ndiyo miongoni mwa makundi yanayoongoza kwa kulipa kodi, akitaka wajibu huo utekelezwe na wadau wengine.
Wanaolipwa kwa mapato ya halmashauri
Makamu huyo wa Rais, alisema Serikali inaendelea na utekelezaji wa kuwaondoa watumishi wanaolipwa kwa vyanzo vya ndani.
Kuanzia Julai 2024, alisema watumishi 473 kutoka halmashauri 101 zilizobainika kutokuwa na uwezo wa kulipa mishahara watumishi wake, watalipwa kwa mfuko mkuu wa Serikali.
Alieleza Sh3.5 bilioni zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo, huku tathmini ya mara kwa mara ikitarajiwa kufanyika ili kubaini uwezo wa kifedha wa halmashauri husika.
Lakini alisema anatarajia halmashauri zitasimamia vema fedha za mapato ya ndani na kutekeleza huduma za kijamii, huku akizitaka kubuni vyanzo vipya na kusimamia matumizi yake.
Ufafanuzi huo, ulitokana na madai ya uwepo wa wafanyakazi wa halmashauri wanaokosa haki kwa kulipwa kwa mapato ya ndani, huku wengine wakilipwa na mfuko mkuu wa Serikali.
Migogoro kazini
Dk Mpango alitumia jukwaa hilo kujibu pendekezo la Tucta lililotaka Serikali iiwezeshe Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwa kuipatia vitendea kazi na kuongeza idadi ya wasuluhishi na waamuzi ili kuboresha huduma zake.
Akijibu hilo, alisema kwa kutambua umuhimu wa CMA, Serikali itaipatia vitendea kazi na kuongeza nguvu kazi ili kuboresha huduma hizo.
Miongoni mwa vitendea kazi hivyo, Dk Mpango alisema ni magari kwa ajili ya usafiri ili kuwafuata walalamikaji wa migogoro ya kikazi walioko mbali na Ofisi za CMA hasa ngazi za Wilaya zisizo na huduma.
Msingi wa ufafanuzi huo ni hoja ya Mkunda kuwa, kumekuwa na ucheleweshwaji wa migogoro ya wafanyakazi, ambayo kimsingi inahitajika kumalizika haraka ili uzalishaji uendelee.
Alisisitiza pamoja na migogoro hiyo mara nyingi kusuluhishwa na mamlaka mbalimbali, ni vema ikarejeshwa CMA kwa uratibu wa kushughulikiwa haraka.
Kurejeshwa SSRA
Risala hiyo ya Tucta, ilipendekeza kurudishwa kwa Mamlaka ya Udhibiti na Uhifadhi wa Mifuko ya Usimamizi ya (SSRA), iliyofutwa tangu mwaka 2018.
Kuhusu hilo, Dk Mpango alisema tathmini ya ushauri huo itaendelea kufanyika kwa kuzingatia maoni ya kitaalamu na uhalisia wa kiuendeshaji kwenye sekta ya hifadhi ya jamii.
Hata hivyo, Dk Mpango, alisema baada ya kupitia na kujiridhisha na yaliyomo ndani ya mikataba ya Shirika la Kazi la Kimataifa (ILO), tayari imeridhia minane nane kati ya 10 na mingine sita ipo katika mchakato wa kuridhia.
Kuridhiwa kwa mikataba hiyo, alieleza kunafanyika baada ya Serikali kujiridhisha kuwa, haikindani na tamaduni, taratibu na tabia za Watanzania.
Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Oscar Mgaya alitumia jukwaa hilo kuomba Serikali itekeleze ahadi yake ya kupunguza Kodi ya Ujuzi na Maendeleo (SDL) kila mwaka hadi itakapofikia asilimia mbili.
“Ni matumaini yetu kuwa ilea hadi ya Waziri wa Fedha katika hotuba yake ya bajeti ya mwaka jana ataikumbuka na kuendelea kupunguza kodi ya SDL kidogo kidogo kila mwaka hadi itakapofika asilimia 2,” amesema.
ILO
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Ukanda wa Afrika Mashariki, Caroline Mugalla alisema tangu Mei mosi ya mwaka uliopita, shirika hilo limetekeleza mafunzo kwa wafanyakazi kuhusu mambo mbalimbali.
Alieleza wanatambua mchango wa Serikali wa kukuza kazi za staha kama ulivyo mpango wa kimataifa wa kuhimiza uwepo wa kazi za staha.
Alisema Tanzania imetumika kama mfano mzuri katika kongamano la ujuzi kwa vijana, kwani mataifa ya Kenya, Malawi na nchi nyingine ili kujifunza mambo mazuri. |
Katikati ya sherehe ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Ta | Katikati ya sherehe ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limetaja mambo tisa yanayowasibu wafanyakazi nchini na kupendekeza utatuzi wake.
Miongoni mwa mambo hayo ni kupandishwa kwa mishahara, usuluhishi wa migogoro, ajira za mikataba, likizo ya uzazi kwa wanawake na marekebisho katika kikokotoo.
Katika sherehe hizo Rais Samia Suluhu Hassan ndiye aliyealikwa kuwa mgeni rasmi na badala yake, aliwakilishwa na Makamu wa Rais Dk Philip Mpango.
Kwa mujibu wa Tucta, kuwepo kwa changamoto hizo tisa, kunakwaza ari na shauku ya ufanyajikazi kwa miongoni mwa wafanyakazi nchini, huku akisisitiza Serikali ichukue hatua kuleta suluhu.
Hayo yameelezwa jijini Arusha leo Jumatano, Mei 1, 2024 na Katibu Mkuu wa Tucta, Henry Mkunda alipokuwa akisoma risala kwa niaba ya vyama vya wafanyakazi wote kwenye sherehe za maadhimisho ya Mei Mosi.
Mishahara
Kauli mbiu ya kitaifa ya maadhimisho hayo ni ‘Nyongeza ya mishahara ni msingi wa mafao bora na kinga dhidi ya hali ngumu ya maisha.’
Risala hiyo kwa mujibu wa Mkunda, iliakisi maneno ya kauli mbiu ikikumbusha nafasi na mchango wa mishahara katika kufikia maisha bora ya wafanyakazi.
Amekiri maboresho mbalimbali ya mishahara kufanyika kwa sekta binafsi na umma, ambayo hata hivyo amedai hayajakidhi hali ngumu ya maisha iliyopo.
Kwa sababu hiyo, Mkunda amesema wafanyakazi wanashindwa kukidhi mahitaji yao na familia.
“Mishahara nadhifu ina uhusiano mkubwa na upatikanaji wa mafao stahiki ya wastaafu, kwani kadri mshahara unavyokuwa mdogo na ndivyo mafao yanavyokuwa finyu,” amesema.
Kuboreshwa kwa viwango vya mishahara, amesema ndiyo namna pekee itakayowezesha kuondokana na mafao kiduchu kwa wastaafu.
Hata hivyo, amependekeza utaratibu wa kupitia upya kima cha chini ya mshahara wa sekta binafsi kila baada ya miaka mitatu unapaswa kuendelezwa.
Katika risalama hiyo, Mkunda amesema dhamira ya Serikali kuongeza posho mbalimbali kwa wafanyakazi inaathiriwa na kodi zinazotozwa kwenye mapato yasiyo ya mshahara.
“Tumeshuhudia wafanyakazi wakikatwa PAYE kwenye posho zote wanazolipwa, nyumba, usafiri, maji, umeme, mawasiliano, samani na muda wa ziada, hizi zinapunguza uwezo wa mtumishi anapokuwa anatumia fedha hizo,” amesema.
Akijibu hilo, Dk Mpango amesema Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara kwa sekta binafsi na umma zipo n zinaendelea na kazi.
Amesema bodi hiyo hasa kwa sekta binafsi ndiyo iliyochangia kufikia uamuzi wa kima kipya cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi kilichotangazwa mwaka 2022 Novemba na kuanza kutumika Januari 2023.
Ameeleza sheria inaitaka bodi ifanye majukumu yake kila baada ya miaka mitatu na amri ya kupitia kima cha chini cha mshahara
Kuhusu hilo, amesema utafiti wa kina wa kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi utakaojumuisha sekta ndogondogo unafanyika.
“Nawasihi wajumbe wa bodi kutoka Tucta mshiriki ili kupata matokeo yatakayoendana na muda sahihi,” amesema.
Migogoro
Akiendelea na risala hiyo Mkunda amesema kumekuwa na migogoro isiyo ya lazima baada ya Serikali kufuta baadhi ya vifungu vya mikataba ya hali bora kwenye taasisi za umma kwa kutumia waraka bila kujali mikataba inayofutwa kwa makubaliano ya pande mbili.
Ametaka mikataba hiyo iendelee kuheshimiwa na kutumika kwa mujibu wa makubaliano ya awali na iwapo kuna mabadiliko uzingatiwe utaratibu wa pamoja.
Kuhusu hilo, Dk Mpango amejibu hakuna ukiukwaji wa sheria uliofanywa na Katibu Mkuu Utumishi katika kuvunjwa kwa vifungu hivyo vya mikataba.
Kilichofanyika amesema ni kwa mujibu wa sheria, inayotaka utekelezwaji wake uzingatie masuala ya kibajeti.
Hata hivyo, amesema ni muhimu kuwepo maslahi kidogo lakini yanayotekelezeka kuliko kuweka makubwa yasiyotekelezeka.
Watumishi halmashauri
Katika risala hiyo, Mkunda aliibua hoja ya uwepo wa wafanyakazi katika halmashauri wanaolipwa kwa mapato ya ndani, badala ya mfuko mkuu wa Serikali.
Utaratibu huo, Mkunda amesema uanwafanya baadhi yao kukosa haki zao za msingi kwa sababu baadhi ya halmashauri zina uwezo mdogo wa kukusanya.
“Mara nyingi wanakosa haki za msingi zikiwemo huduma za afya, mafao ya ustaafu na hata kushindwa kuwasilisha michango yao,” amesema.
Amependekeza umuhimu wa Serikali kubadili utaratibu huo na kutoa haki kwa kila mfanyakazi alipwe na mfuko mkuu.
Katika hoja hiyo, Dk Mpango amesema Serikali inaendelea na utekelezaji wa kuwaondoa watumishi wanaolipwa kwa vyanzo vya ndani.
Kuanzia Julai mwaka huu, amesema watumishi 473 kutoka halmashauri 101 zilizobainika kutokuwa na uwezo wa kulipa mishahara watumishi wake, watalipwa kwa mfuko mkuu wa Serikali.
Ameeleza Sh3.5 bilioni zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo, huku tathmini ya mara kwa mara ikitarajiwa kufanyika ili kubaini uwezo wa kifedha wa halmashauri husika.
Lakini amesema anatarajia halmashauri zitasimamia vema fedha za mapato ya ndani na kutekeleza huduma za kijamii, huku akizitaka kubuni vyanzo vipya na kusimamia matumizi yake.
SSRA irudishwe
Risala hiyo pia kwa mujibu wa Mkunda, iliibua hoja ya kurudishwa kwa Mamlaka ya Udhibiti na Uhifadhi wa Mifuko ya Usimamizi ya (SSRA), iliyofutwa tangu mwaka 2018.
Amesema tangu kufutwa kwake, kumeundwa kitengo chini ya wizara husika na ajira kwa ajili ya kudhibiti na kusimamia mifuko ya hifadhi ya jamii, akisema si jambo jema.
Amependekeza umuhimu wa kurudishwa kwa SSRA kwa kuwa ilipokuwepo ilikuwa na manufaa kwa wafanyakazi.
“Utaratibu wa sasa haukidhi malengo yaliyokusudiwa kwa kuwa Serikali ni mhadhimi wa mifuko na wakati huo huo inakuwa mdhibiti na msimamizi wa mifuko,” amesema.
Kikokotoo
Kwa mujibu wa Mkunda, mwaka 2022 yalifanyika mabadiliko kwenye kanuni za kukokotoa mafao ya wafanyakazi wastaafu wa umma na binafsi.
Katika hilo, ameishukuru Serikali kwa hatua ya kuwashirikisha wafanyakazi katika mchakato huo, tofauti na ilivyofanyika awali.
Pamoja na yote hayo, amesema miaka miwili tangu utekelezwaji ulipoanza, tathmini ndogo imeonyesha wafanyakazi hawaridhishwi na kanuni mpya za kukokotoa mafao ya wastaafu.
Kwa kuwa mifuko inaonekana kuimarika sasa, amependekeza kanuni hizo ziboreshwe na kuleta mafao bora kwa wastaafu bila kuathiri mifuko hiyo.
Ajira za mikataba
Katika risala hiyo pia, amedokeza uwepo wa ajira za mikataba zinazotolewa kinyume na matakwa ya sheria ya ajira na mahusiano kazini.
Amesema ajira hizo ni za mikataba ya miezi mitatu na nyingine mwaka mmoja na zimekuwa zikitolewa kwa mfululizo.
Hata hivyo, amesema wanaoajiriwa katika ajira hizo si wale wataalamu na mameneja pekee kama walivyotambuliwa na sheria, bali makundi mengine mbalimbali huajiriwa.
“Tumeshuhudia katika taasisi za umma na sekta binafsi zikitoa ajira za mikataba ya miezi mitatu au mwaka mmoja kwa wafanyakazi kwa kipindi kirefu kwa wafanyakazi kwa mfululizo kwa mtumishi,” alisema.
Alisema uwepo wa ajira za mikataba hiyo mifupi kwa mtumishi kwa kipindi kifupi unaonyesha upo uhitaji wa ajira za kudumu, au za muda mrefu katika eneo husika.
Bima ya afya
Katika risalama hiyo, Mkunda ameeleza uwepo wa malalamiko ya wafanyakazi juu ya kutoshirikishwa katika maboresho ya kitita cha mafao, yaliyofanyika tangu mwaka 2023 na kuanza kutumika mwaka huu.
Amesema utaratibu wa mfuko kusitisha huduma za bima ya afya kwa wachangiaji na wategemezi pale mwajiri anapochelewesha mchango ni makosa.
Makosa yanatokana na kile alichoeleza, mfanyakazi anakuwa ameshakatwa mshahara wake na makato yote ya kisheria hivyo jukumu la kufikisha kwa michango ni la mwajiri.
Alipendekeza mfanyakazi aendelee kupata huduma na asiathiriwe kwa kosa la mwajiri la kutowasilisha michango.
Utatuzi migogoro
Amesema kuna haja ya kuboresha sheria na taratibu za kusuluhisha migogoro ya wafanyakazi ili waendelee kuzalisha, badala ya ilivyo sasa muda mwingi hutumika bila matatizo kuisha.
Ametaka kuongezwa kwa bajeti na kuwezeshwa kwa CMA ili iwe na uwezo wa kutatua migogoro hiyo haraka.
Likizo
Mkunda amemomba Dk Mpango kuongeza miezi mitatu ili iwe sita kwa ajili ya likizo ya uzazi kwa wanawake wanapokwenda kujifungua.
Amesema kufanya hivyo, kutajenga afya ya akili ya mfanyakazi na malezi bora ya mtoto, tofauti na sasa ambapo mwanamkie akienda likizo ya uzazi anakuwa na hofu ya kibarua chake. |
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ameonyesha hofu ya kuzungumza mambo mengi mbele ya Makamu wa Ra | Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ameonyesha hofu ya kuzungumza mambo mengi mbele ya Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango kwa kile alichoeleza, akifanya hivyo atayakoroga.
Hofu yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, yupo katika furaha na katika nyakati kama hizo akizungumza zaidi atayakoroga.
Kauli yake hiyo inakuja wakati ambao, Makonda amekuwa na historia ya kutoa kauli mbalimbali zinazoibua mijadala na hata kusababisha mashaka ndani ya Serikali.
Mwanzoni mwa Aprili mwaka huu, Makonda aliahidi kuwataja Mawaziri wanaoshiriki kulipa na kutuma watu wanaomtukana Rais Samia Suluhu Hassan mitandaoni.
Kauli yake hiyo, ilimsababisha kuitwa na Kamati ya Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kumhoji kwa takriban saa tatu.
Makonda ameonyesha hofu hiyo leo Jumatano, Mei 1, 2024 alipotoa salamu za Mkoa wa Arusha katika Sherehe za Sikukuu ya Wafanyakazi kitaifa.
Katika hotuba yake hiyo Makonda alimwomba Dk Mpango amruhusu kuzungumza mambo machache kati ya mengi aliyonayo kwa hofu kuwa, furaha aliyonayo itamfanya akoroge mambo.
“Hapa nitakoroga mambo Mheshimiwa makamu wa Rais uniruhusu niseme matatu, ukiwa na furaha sana unaweza ukajikuta unasema mambo mengi,” amesema.
Mambo hayo matatu aliyoyasema ni pongezi kwa Rais Samia kwa mchango wake katika sekta ya utalii unaosababisha matarajio ya ujio wa watalii wengi watakaofaidisha wananchi.
Jambo la pili, amesema ni ombi kwa Serikali kuu kuwezesha maboresho ya barabara katika Jiji hilo, kwa kuwa zilizopo hazipitiki kwa urahisi.
Kwa mujibu wa Makonda, sherehe hizo zinafanyika katika wakati ambao Tanzania inadumisha umoja na kwamba hatatokea yeyote wa kuligawanya taifa. |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametaka uwazi na usimamizi madhubuti wa fedha katika utekelezwaji wa mi | Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametaka uwazi na usimamizi madhubuti wa fedha katika utekelezwaji wa miradi ya umwagiliaji nchini.
Majaliwa ametoa maelekezo hayo kwa watendaji watakaohusika na usimamizi wa miradi hiyo, akisisitiza kufanya hivyo kutachagiza kukamilika haraka kwa kazi hizo.
Kauli ya Mtendaji Mkuu huyo wa Serikali inakuja katika kipindi ambacho, Serikali imeweka dhamira ya kutekeleza miradi lukuki ya umwagiliaji ili kuboresha sekta ya kilimo.
Katika maboresho hayo ya sekta ya kilimo, Serikali imeweka dhamira ya kuhakikisha inaongeza mchango katika pato la taifa kutoka asilimia 26 hadi 50 mwaka 2030.
Majaliwa ameyasema hayo jijini Dodoma leo Jumanne, Aprili 30, 2024 alipohutubia katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya ujenzi, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa miradi ya umwagiliaji.
Amesema ni muhimu watendaji watakaohusika na usimamizi wa miradi hiyo kuzingatia ufanisi na usimamizi imara wa fedha ili kazi zifanyike kwa haraka.
Pamoja na ufanisi, Majaliwa ametaka uwazi katika utekelezaji wa miradi hiyo, ili kuepuka ubadhirifu wa fedha na miradi kutekelezwa kinyume na matarajio.
“Fedha hizo ni kodi za wananchi wa Tanzania, zitumike kuwanufaisha Watanzania wote,” amesema.
Agizo lingine alilolitoa kupitia jukwaa hilo ni watendaji hao kuhakikisha ubora wa miradi unalingana na thamani halisi ya fedha iliyotolewa kwa ajili ya utekelezaji.
Lakini, ametaka kwa miradi itakayotekelezwa kwa njia ya Force Account kipaumbele cha ajira kitolewe kwa wananchi wa jirani na maeneo ya utekelezwaji.
Katika hatua nyingine, Majaliwa amesema serikali imedhamiria kusimamia kilimo cha umwagiliaji ndiyo maana imeongeza bajeti kufikia Sh361.5 bilioni mwaka 2023/2024 kutoka Sh46.5 bilioni ya mwaka 2021/2022.
“Matarajio ya Serikali ni kuona miradi inayotekelezwa itakamilika kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa ili kuwezesha kutimia kwa azma ya Serikali ya kuongeza mchango wa sekta ya kilimo katika Pato la Taifa,” amesema.
Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema mikakati ya Serikali ni kuanza kutumia maji ya Ziwa Tanganyika katika miradi ya kilimo cha umwagiliaji.
Hilo, amesema litaanza na Mikoa ya Katavi na Rukwa na baada ya Bunge la bajeti, upembuzi wa kina na yakinifu utafanyika ili maji hayo yasafirishwe hadi Simiyu na Tabora, maeneo ambayo aghalabu huwa na ukame.
"Baada ya Bunge la bajeti kukamilika tunatarajia kuanza kuyatumia maji ya ziwa Tanganyika katika shughuli za kilimo na uzuri mitambo tunayo naamini jambo hili litafanikiwa," amesema.
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) Raymond Mndolwa amesema mikataba mikataba 24 imesainiwa na kati ya hiyo, 14 ya ujenzi kwa kutumia wakandarasi yenye thamani ya Sh248.7 bilioni, sita ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kutumia Washauri Elekezi yenye thamani ya Sh9.35 bilioni.
Miradi minne, amesema itatekelezwa kwa kutumia wataalamu wa ndani kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji yenye thamani ya Sh16.95 bilioni. |
Ili kuimarisha utaalamu na mbinu za kisheria katika kukabiliana na uhalifu wa mtandao, Serikali inas | Ili kuimarisha utaalamu na mbinu za kisheria katika kukabiliana na uhalifu wa mtandao, Serikali inashirikiana na Urusi kubadilishana uzoefu na elimu juu ya masuala hayo.
Katika kufanikisha hilo, wataalamu kutoka Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Urusi wamewasili nchini na kutoa mafunzo kwa wanafunzi na wanataaluma ya sheria kuhusu masuala hayo.
Ushirikiano wa mataifa hayo kuhusu masuala ya kisheria ni matokeo ya ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mawaziri wengine kwenda Urusi Julai mwaka jana.
Katika ziara hiyo ya mwaka jana, pamoja na mambo mengine viongozi hao walisaini hati mbalimbali za makubaliano ikiwemo ya ushirikiano wa kisheria katika kukabiliana na uhalifu wa mtandao na ugaidi.
Mafunzo kuhusu masuala hayo yamefanyika jana, katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), jijini Dar es Salaam.
Akifungua muhadhara wa wataalamu hao kutoka Urusi, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Pindi Chana alisema hiyo ni hatua muhimu katika kuyafikia malengo ya dunia.
Alieleza mafunzo hayo yanalenga kujenga uwezo wa utaalamu wa kisheria kwa wanataaluma hiyo waliopo nchini, ili wamudu kukabiliana na uhalifu ukiwemo wa mtandao na ugaidi.
“Mafunzo haya yanalenga kuondoa changamoto za kisheria zinazoyakabili mataifa mbalimbali duniani na kwamba hii ni fursa ya kubadilishana uzoefu. Hili ni jambo muhimu kwa sababu muelekeo wa dunia ni mmoja, Dunia yote inapambana dhidi ya kukandamizwa kwa haki za binadamu na uhalifu,” alisema.
Katika hotuba yake hiyo, alisisitiza kinachofanyika ni matokeo ya makubaliano kati ya Tanzania na Urusi na kwamba kuna maeneo mengine ya ushirikiano yatakayoongezwa.
Kwa mujibu wa Dk Chana, msingi wa mafunzo na ushirikiano huo ni kuimarisha misingi ya haki na usawa katika jamii ya Tanzania.
Awali, akihutubia muhadhara huo, Mkuu wa Taasisi LST, Profesa Sist Mramba alisema kunahitajika ushirikiano wa kimataifa ili kukabili ugaidi na uhalifu wa kimtandao.
“Changamoto zinazoikabili dunia kwa sasa ni ugaidi na uhalifu wa mtandao, kunahitajika ushirikiano wa mataifa mbalimbali katika kupeana ujuzi ili kukabiliana na changamoto zilizopo,” alisema.
Msisitizo wa hoja yake hiyo ni kile alichoeleza, kujenga uelewa wa kisheria juu ya kukabiliana na majanga ya uhalifu ukiwemo wa mtandao.
Balozi kutoka Shirikisho la Urusi nchini, Andrey Avetisyan alielezwa kufurahishwa na hatua kubwa za kimageuzi katika mifumo ya kisheria zilizopigwa Tanzania.
Kadhalika, alisema anafurahishwa na mazingira rafiki na mazuri yanayowekwa na Serikali na Tanzania katika uwekezaji na biashara, huku akiwahimiza wawekezaji kutoka Urusi kuja kuwekeza nchini.
Hata hivyo, alisema ushirikiano wa Urusi na Tanzania hasa katika masuala ya kisheria utajenga uelewa na mbinu bora za kukabiliana changamoto zilizopo.
Alieleza kuna umuhimu mkubwa wa ushirikiano wa kisheria kwani unawezesha kujua mifumo ya kisheria ya kila taifa na hata kufahamu sheria zilizopo.
Kwa mujibu wa Balozi huyo, ushirikiano wa kisheria ni muhimu hata kwa sasa kwa mustakabali wa uhusiano baina ya mataifa hayo.
Alieleza Urusi ipo Tanzania kuendelea kufurahia ushirikiano, huku alimwalika Dk Pindi kwenye Jukwaa la Kisheria la St. Peter litakalofanyika Juni nchini humo.
Alisisitiza ushirikiano huo hautaishia hapo, utakwenda mbali Zaidi hadi katika kubadilishana wanafunzi wa sharia kati ya Tanzania na Urusi. |
Rais Samia Suluhu Hassan amesema ili kuziwezesha nchi za Afrika kuwa na maendeleo shindani duniani, | Rais Samia Suluhu Hassan amesema ili kuziwezesha nchi za Afrika kuwa na maendeleo shindani duniani, ni muhimu taasisi za fedha za kimataifa zizingatie utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu.
Msisitizo wa mkuu huyo wa nchi katika hoja yake hiyo ni kuzitaka taasisi za fedha za kimataifa kurahisisha masharti ya mikopo yake ili nchi za Afrika zijiinue kimaendeleo.
Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, Aprili 29, 2024 alipohutubia mkutano wa 21 wa wakuu wa nchi wa Shirikisho la Kimataifa la Maendeleo (IDA), jijini Nairobi nchini Kenya.
Katika hotuba yake hiyo, amesema nchi za Afrika na Dunia kwa ujumla zipo katika kipindi ambacho, majanga mbalimbali yanayanazikabili.
Katika kufanikisha ukuaji wa maendeleo shindaji hasa kwa nchi za Afrika ametoa wito kwa IDA kufanikisha utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu.
Amekwenda mbali zaidi na kusisitiza upatikanaji wa mikopo yenye masharti ya kulipa baada ya miaka 50.
“Kwa kuzingatia changamoto zilizopo, naamini IDA itaendelea na utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu zaidi kama vile ile ya kulipa ndani ya miaka 50. Uwezeshaji huu unatoa nafasi zaidi kwa Afrika kushindania mahitaji ya maendeleo,” amesema.
Amesema Afrika inahitaji uahaulishaji wa teknolojia na namna ya kuzitumia ili ifikie maendeleo yanayotarajiwa na shirikisho hilo, huku akirejea fursa ambazo Tanzania imezipata kupitia IDA.
Ametaja miongoni mwa fursa hizo ni mpango wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya Bonde la Msimbazi ambao Benki ya Duni imetoa Dola milioni 2 za Marekani.
Sambamba na mradi huo, amesema shirikisho hilo limeinufaisha Tanzania kwa kuiwezesha kuboresha huduma za afya ya uzazi, ufikishaji wa huduma ya umeme vijijini na kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama.
Ameeleza mkutano huo unakuja katika kipindi ambacho sera na mipango imeboreshwa kurahisisha utekelezwaji wa shughuli mbalimbali.
Matarajio yake, amesema IDA iziwezeshe baadhi ya nchi kukua kiuchumi na maendeleo.
Wataka uwezeshaji mabadiliko tabianchi
Viongozi wengine wa Afrika wamezisisitiza nchi tajiri kutoa michango kwa Benki ya Dunia ili kuiwezesha kutoa misaada kwa nchi zinazoendelea kwa ajili ya kusaidia maendeleo na kukabili athari za mabadiliko ya tabianchi.
Nchi hizo tajiri zinatarajiwa kutoa ahadi ya michango yao kwa IDA katika mkutano utakaofanyika Japani Desemba, mwaka huu.
"Tunatoa wito kwa washirika wetu kuhakikisha wanaongeza michango yao ndani ya IDA... angalau ifikie Dola za Marekani 120 billioni," amesema Rais wa Kenya, William Ruto katika mkutano wa IDA jana.
Katika hotuba yake alisema, uchumi wa nchi za Afrika umetikisika kutokana na madeni na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayohitaji hatua za haraka kujiokoa.
Alitolea mfano taifa lake la Kenya linakabiliwa na mafuriko yaliyopitiliza huku mengine ya Kusini mwa Afrika yakikabiliwa na ukame ikiwemo Malawi.
Iwapo wadau hao wataahidi kiwango hicho kilichopendekezwa na viongozi wa Afrika, kitakuwa cha kwanza kwa ukubwa tangu ahadi zilizowahi kutolewa mwaka 2021 zilizoishia Dola za Marekani 93 bilioni.
IDA inatoa mikopo yenye riba nafuu kwa nchi 75 zinazioendelea duniani na zaidi ya nusu zinatoka Afrika.
Fedha hizo kwa mujibu wa benki ya dunia, zinatumika na Serikali za nchi hizo, kugharimia upatikanaji wa nishati na huduma za afya, uwekezaji kwenye kilimo na kujenga miundombinu ikiwemo ya barabara.
Rais wa Benki ya Dunia, Ajay Banga alitumia jukwaa hilo la IDA ya 21 kuahidi kuondoa vikwazo vyote vinavyotatiza ukopaji ili kuongeza ufanisi na urahisi katika utolewaji wake.
"Tunaamini IDA ikiwa rahisi inaweza kuleta matokeo makubwa na yenye maana zaidi ukilinganisha na kuweka mazingira magumu,” alisema Banga. |
Utunzaji wa uoto wa asili kwenye maeneo yenye miinuko mikubwa ni moja ya mbinu zilizotajwa na wataal | Utunzaji wa uoto wa asili kwenye maeneo yenye miinuko mikubwa ni moja ya mbinu zilizotajwa na wataalamu za kupunguza hatari ya kutokea kwa maporomoko ya tope, baada ya mvua nyingi.
Kwa mujibu wa wanazuoni hao waliobobea katika taaluma ya jiolojia na miamba, ingawa matukio hayo si rahisi kuyadhibiti, angalau kuepuka kujenga juu ya miinuko au mabondeni kunaweza kuepusha madhara tarajiwa.
Mitazamo ya wasomi hao, inakuja katika kipindi ambacho baadhi ya maeneo nchini yameathiriwa na maporomoko ya tope baada ya mvua zilizonyesha kwa miezi saba mfululizo.
Aprili 14, 2024, shule tano ililazimika zifungwe kwa muda baada ya kufunikwa na tope lililoporomoka kutoka Mlima wa Kawetele katika Kata ya Itezi jijini Mbeya.
Shule hizo ni Tambukareli, Mary’s, Mafanikio, Itezi na Generation kwa mujibu wa Anderson Mwalongo Ofisa Elimu, Vifaa na Takwimu katika Jiji hilo.
Hali kama hiyo ilitokea wiki iliyopita katika Mlima wa Kabumbilo kwenda Mwaloni wilayani Muleba mkoani Kagera na kuathiri zaidi ya ekari 10 za mashamba ya wananchi, baada ya kufunikwa na tope hilo.
Kama hiyo haitoshi, wananchi kadhaa walipoteza makazi yao wilayani Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro, baada ya nyumba zao kufunikwa na tope.
Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, wanazuoni hao walipendekeza kuepuka ujenzi na uendelezaji kwenye mabonde linakokimbilia tope hilo na kwenye milima linakotokea, ni hatua muhimu zinazopaswa kuchukuliwa.
Ni hali inayojirudia
Mwanazuoni wa Uhandisi katika Jiolojia na Utaalamu wa Miamba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Mhadhiri Dk Kenneth Lupongo anasema kuna uwezekano mkubwa wa matukio hayo kujirudia katika maeneo yaliyotokea.
Uwezekano huo unatokana na kile alichofafanua, eneo lilikotokea tukio hilo mara nyingi hukosa msawazo na inabidi hali ijirudie ili lipate kile alichokiita equilibrium (usawa).
“Mara nyingi kwenye eneo lilipotokea huwa linajirudia hadi eneo hilo litakapopata Equilibrium (msawazo). Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa wa tukio kujirudia,” anasema Dk Lupongo.
Mvua sio sababu pekee
Ingawa mvua nyingi ni moja ya sababu za kutokea kwa hali hiyo, mhadhiri huyo anasema zipo sababu nyingine tatu zinazochagiza tukio hilo.
Anazitaja sababu hizo ni tetemeko la ardhi, milipuko ya volcano na shughuli za binadamu katika maeneo yasiyopaswa, hasa yenye miinuko.
Kuhusu mvua, anasema mmomonyoko huo hutokea pale udongo unapobeba maji mengi na kushindwa kustahimili hivyo unaporomoka.
Kwa upande wa shughuli za binadamu kwa mujibu wa Dk Lupongo, zinahusisha ukataji wa miti na ujenzi na uendelezaji wa maeneo yasiyopaswa kuendelezwa.
“Matukio haya hutokea kwenye maeneo yenye miinuko mikubwa na kwa Tanzania inajulikana. Maeneo hatari kwa Tanzania ni miinuko ya Usambara, Pale, Kilimanjaro, Meru, Hanang, Uruguru, Mbeya na karibu na mipaka ya Burundi na Rwanda,” anasema.
Kujenga uelewa juu ya uwepo wa matukio kama hayo katika maeneo yenye miinuko ni miongoni mwa mapendekezo ya mwanazuoni huyo ili kukabiliana na hali hiyo.
Anaeleza iwapo maeneo hayo yatajulikana itakuwa rahisi kuyafuatilia na kudhibiti hali kabla ya madhara, kwa sababu hayatokei kwa kushtukiza.
“Ni muhimu kujua tabia za maeneo yenye miinuko ili kuepuka kufanya shughuli yoyote au kama inafanywa basi tahadhari ichukuliwe,” anaeleza.
Nguvu kudhibiti
Mtaalamu mwingine wa Jiolojia na miamba, Profesa Shukurani Manya anasema ni vigumu kudhibiti hali hiyo katika mazingira ambayo mvua nyingi zimenyesha.
“Maporomoko ya udongo katika miinuko, yanatarajiwa wakati mvua zinapokuwa nyingi na hayadhibitiki. Ardhi ikinyonya maji mengi kuliko kawaida lazima udongo huo ushuke,” anasema.
Lakini, kuna uwezekano wa kupunguza athari za hali hiyo, kwa mujibu wa Profesa Manya.
Anasema hilo litawezekana iwapo uoto wa asili kama vile nyasi na miti inayokuwepo kwenye miinuko hiyo, isikatwe ili kuruhusu maji kunyonywa taratibu.
“Pia, watu wasipende kujenga katika maeneo hayo au chini ya miinuko hiyo na katika njia za mserereko wa udongo ili kupunguza uharibifu wa mali,” anaeleza.
Mbinu kudhibiti
Msisitizo wa mwanazuoni huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kupunguza shughuli za kibinadamu katika sehemu za miinuko na chini yake.
Kufanya hivyo, anasema kutaruhusu uoto wa asili na miti kuota na hivyo kuimarisha kushikiliwa kwa udongo na maji ya mvua kunyonywa taratibu.
Mtazamo wa Profesa Manya ulishabihiana na mwanazuoni mwingine katika eneo hilo, Profesa Maboko Makenya aliyesema inawezekana kupunguza ukubwa kwa kuhifadhi mazingira, lakini si kudhibiti kabisa.
Kwa mujibu wa Profesa Makenya, mvua zinapokuwa nyingi na udongo ukatepeta, wakati mwingi hata kama kuna miti ya kutosha inang’olewa na hali hiyo.
“Hii hali ikitokea wakati mwingine inang’oa hadi miamba si miti pekee, kwa hiyo ni muhimu kutunza mazingira kwa kupanda miti ili kupunguza kiwango cha athari lakini si kudhibiti kabisa,” anasema.
Jambo muhimu, anasema ni wananchi kuhakikisha hawaweki makazi katika maeneo yenye miinuko mikubwa na mabonde kwa kuwa mmomonyoko unapotokea hukimbilia huko. |
Licha ya uwepo wa daraja la Zingiziwa katika Mtaa wa Zingiziwa wilayani Ilala, Dar es Salaam safari | Licha ya uwepo wa daraja la Zingiziwa katika Mtaa wa Zingiziwa wilayani Ilala, Dar es Salaam safari ya kutoka mtaa huo kwenda mwingine imekuwa kikwazo.
Hiyo inatokana na mvua zinazoendelea kunyesha eneo hilo na mengine nchini, zilizosababisha daraja hilo kujaa maji na sasa yanapita juu.
Kwa mujibu wa watumiaji wa daraja hilo, hali iliyopo sasa ni zaidi ya ile iliyokuwepo jana, huku Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) ikitabiri kuendelea kwa mvua hizo hadi Jumapili (keshokutwa).
Mwananchi Digital imeshuhudia wananchi wakipata tabu kuvuka katika eneo hilo, wengi wakishikwa mkono ili kuwaepusha wasisombwe na maji na kwa msaada huo walilazimika kuulipia Sh500.
Mbali na wananchi, maofisa wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) waliokuwa safarini kwenda kutengeneza transfoma iliyolipuka, nao walilazimika kuvushwa kwa utaratibu huo.
Hakuna gari wala pikipiki iliyokuwa inavuka katika eneo hilo, badala yake kila mwenye chombo chake cha usafiri aliishia kuiacha ng’ambo na kuvuka kwa mguu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika eneo hilo leo Ijumaa, Aprili 26, 2024 wananchi hao wamesema hali hiyo imekwaza shughuli zao.
Kujaa maji kwa daraja hilo, kulimlazimu Lulu Mkeni mkazi wa Lukabaya kulipia Sh500 ili avushwe kwenda zilipo ofisi za Mtendaji wa Kata kupeleka barua ya maombi ya kazi.
"Serikali itengeneze eneo hili kwa kuwa kila mvua zikinyesha hali imekuwa ndio hii, hebu itimize ahadi yake nasi tupate ahueni, tunalazimika kuvuka kwa sababu tuna mahitaji upande wa pili,” amesema.
Hali hiyo ilikwamisha safari ya Mohammed Awadhi dereva wa bodaboda kutoka Kariakoo, aliyekuwa na abiria wake anayepaswa kumpeleka nyumbani kwake ng’ambo ya daraja hilo.
"Inabidi tu nisubiri hadi maji yatakapopungua ili nimvushe mteja wangu yupo na mizigo mingi hawezi kuvuka nayo," amesema.
Kutokana na kujirudia kwa changamoto hiyo, Maria Makamburi anayetumia daraja hilo, amependekeza kujengwa kwa daraja kubwa zaidi.
Amesema changamoto zinazoendelea katika eneo hilo, zinasababisha hata wanafunzi washindwe kwenda shuleni.
Mwananchi mwingine, Halima Ramadhani amesema changamoto si daraja hilo pekee, hata barabara ni mbovu, akiisisitiza Serikali ifanye ujenzi.
Wengine furaha
Wakati wengine wakilalamikia madhila hayo, kwa baadhi ya vijana ilikuwa kicheko wakitaka Serikali ialiache eneo hilo kama lilivyo.
Sababu ya tamanio lao hilo ni kile alichoeleza, wanajipatia fedha kwa kuvusha watu kutoka upande mmoja kwenda mwingine.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Zingiziwa, Mohamed Kirungi amesema tayari Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo alishafika kwenye eneo hilo kuona hali ilivyo.
“Tunaomba hatua zichukuliwe haraka,” amesema.
mwisho.
Ili kuuenzi na kudumisha muungano kwa miaka 60 ijayo, wadau wameshauri somo kuhusu jambo hilo lianzishwe na kufundishwa shuleni kuanzia ngazi ya chini.
Pendekezo hilo, lilitolewa jana na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Mohamed Khartoum alipozungumza na Mwananchi kuhusu maadhimisho ya miaka 60 ya muungano.
Katika maelezo yake, alisema hatua ya kufikiwa kwa miaka 60 ya muungano si ndogo hivyo juhudi zaidi zinahitajika ili uendelee kudumu kama ilivyokusudiwa.
Kwa kuwa idadi kubwa ya watanzania wa sasa wamezaliwa baada ya muungano, alipendekeza jambo hilo lifanywe kuwa somo ili kuambukiza maarifa kwa kizazi kijacho.
“Sasa hivi elimu kuhusu Muungano inatolewa wakati wa maadhimisho tu na baada ya hapo kila kitu kinaishia lakini kama somo maalumu likiwepo na kufundishwa kila Mtanzania aliyeko Bara na Zanzibar atajua umuhimu wake kuulinda kwa hali na mali.
“Kwa sasa linafundishwa shuleni kama mtalaa kwa ajili ya kujibu katika mtihani kuwa Muungano ulifanyika Aprili 26, 1964 ili watu kupata alama nzuri za ufaulu lakini baada ya hapo hakuna anayejua zaidi kuhusu umuhimu na kwa nini nchi hizi mbili ziliungana,” alisema Dk Khartoum.
Kwa mujibu wa mwanazuoni huyo, suala la Muungano kwa sasa limeachwa mikononi mwa wanasiasa wanaolisemea ili kupata alama wakati wa kuzungumza, ingawa kuna wakati mwingine wanapotosha.
“Kwa mfano juzi kuna mbunge ametaka kuingia Zanzibar iwe ni kwa hati ya kusafiria kauli iliyoleta taharuki kwa watu wengi lakini ukiangalia hiyo ilikuwa zamani na sasa wameiondoa, sasa mtu akisikia hivyo ni lazima auchukie Muungano kwa kudhani kuna ubaguzi wakati wa kwenda upande wa pili wa Muungano,” alisema Dk Khartoum.
Aprili 23 akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa mwaka 2024/25, mbunge wa Konde, Mohamed Said Issa alishauri kurejeshwa kwa utarativu wa kuingia Zanzibar kwa hati ya kusafiria.
Alisisitiza kama kweli Serikali imedhamiria Muungano uendelee na kudumu lazima iweke nguvu ya ziada ya kuwaelimisha watoto kuhusu suala hilo ili kujua ukweli si kwa kuusikia tu bali kwa kufundishwa na ikitokea mtu anaposha basi wajue jinsi ya kumjibu.
Mbali na hilo, alishauri wizara inayoshughulikia masuala ya Muungano kuleta vipindi vya elimu kwa waliomaliza shule ili kujua suala hilo kupitia redio na vyombo vingine vya habari.
“Nikiwa mmoja wa wanufaika wa Muungano na familia yangu tumeweza kufanya kazi na kupewa haki sawa bila ubaguzi kama Watanzania wengine wanaofanya kazi kwenye taasisi za umma na binafsi,” alisema.
Hata hivyo, Dk Khartoum alisema Muungano una manufaa makubwa ambayo kama akitaka kuyaelezea hataweza kuyamaliza kuanzia ngazi za kijamii, kielimu, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi.
Alisema waasisi wa Muungano huo, Hayati Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume walikuwa na nia nzuri ya kuungana hivyo ni lazima utunzwe kama mboni ya jicho.
“Unajua mtu anapokuwa na macho mawili hawezi kujua athari za kuwa na jicho moja mpaka pale atakapopoteza jicho moja halafu asiweze kuona upande wa pili mpaka ageuke ndipo anapojua thamani ya macho yote mawili, sasa sisi tusifike huko tuulinde muungano wetu kwa hali na mali.” amesema.
Alisema kero za Muungano zilizopo zinazungumzika na hazina madhara makubwa ya kuhatarisha Muungano kwa sababu pamoja na kuwepo lakini mazungumzo ya pande zote mbili yanaendelea.
“Kwenye Muungano wa aina yoyote ile lazima kunakuwa na kutokuelewana kwenye baadhi ya mambo kwa hiyo hizi kero na changamoto zilizopo zisitugawe kwa sababu faida ni kubwa kuliko hizo changamoto zilizopo,” alisema.
Hivi karibuni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dk Seleman Jafo alisema kero nne ikiwemo ya uletaji wa sukari kutoka kiwanda cha Mahonda Zanzibar kuja Tanzania Bara ni miongoni mwa mambo ambayo bado hayapatiwa ufumbuzi.
Kagera
Sherehe za muungano ziliadhimishwa tofauti katika Mkoa wa Kagera, badala ya kufanyika mkutano na viongozi kuzungumza, Serikali mkoani humo ilikusanya wananchi waliochangia damu kiasi cha uniti 51.
Mratibu wa Damu Salama Bukoba, Jastine Jems alisema “chupa za damu uniti 51 tumezipata ni tunashukuru wote walioshiriki uchangiaji huu tulizokusanya kama manispaa”alisema.
Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Erasto Sima aliwataka wananchi wote wanaoshi mkoa huo, kuendelea kuuenzi Muungano kwa kufanya kazi na kushiriki katika huduma za kijamii ikiwemo kuchangia damu salama, badala ya kusubiri kusukumwa bali wajitolea mara kwa mara. |
Rais Samia Suluhu Hassan amesema tathmini zinaonyesha Tanzania ipo mbioni kufikia uchumi wa kati nga | Rais Samia Suluhu Hassan amesema tathmini zinaonyesha Tanzania ipo mbioni kufikia uchumi wa kati ngazi ya juu, kutokana na mwenendo mzuri wa ukuaji uchumi.
Mkuu huyo wa nchi amedokeza hilo, katika kipindi ambacho Tanzania imetambuliwa na Benki ya Dunia (WB), kuwa na uchumi wa kati ngazi ya chini.
Kwa tafsiri za kiuchumi, kuongezeka kutoka hadhi ya chini hadi hadhi ya juu ya uchumi wa kati ni hatua ya kila Mtanzania kufikia uwezo wa wastani wa kipato cha zaidi ya Dola 2,000 za Marekani (zaidi ya Sh5 milioni) kwa mwaka.
Julai mwaka 2020, WB ilitoa taarifa inayoonyesha kupanda kwa hadhi ya uchumi wa Tanzania kutoka chini hadi kipato cha kati ngazi ya chini. Hata hivyo, wastani wa kipato cha kila Mtanzania ni Sh2.5 milioni kwa mwaka.
Rais Samia alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, alipohutubia sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika katika Uwanja wa Uhuru.
Katika hotuba yake hiyo, Rais Samia alisema ishara ya kuimarika kwa muungano ni kuimarika kwa uchumi wa Tanzania kulikotokana na mwenendo mzuri.
Hali hiyo, alieleza inafanya tathmini mbalimbali zionyeshe Tanzania ipo mbioni kupanda hadhi ya kiuchumi kutoka wa kati ngazi ya chini hadi ngazi ya juu.
"Tathmini zinaonyesha Tanzania inakaribia kufikia uchumi wa kati ngazi ya juu kutoka ngazi ya chini tuliyopo sasa," alisema.
Atabiri kupatikana CDF mwanamke
Katika hotuba yake hiyo, Rais Samia alipongeza hatua ya onyesho la askari hao kabla ya muungano, kuwa na mwanamke.
Alisema mara nyingi, katika onyesho hilo, huwa kunakuwa na askari wanaume pekee kwa kuwa wanawake walikuwa wanahofu.
"Nimefurahishwa na hatua ya kuona mwanamke katika onyesho la Paradushi, mara nyingi huwa hatuwezi zile purukushani," alisema.
Kwa dalili hizo, Rais Samia alisema huenda mwaka 2030 Tanzania ikawa na Mkuu wa Majeshi mwanamke.
"Msije mkashangaa 2030 tukawa na CDF (mkuu wa majeshi) mwanamke, inawezekana kama wameanza kwenye onyesho hili," alisema.
Pamoja na kulidokeza hilo, Mkuu huyo wa nchi aliwataka Watanzania kujivunia muungano kwa kuwa umetokana na uamuzi wa wananchi wenyewe.
Alieleza majivuno hayo pia yanahalalishwa na amani na ulinzi uliodumishwa tangu miaka 60 iliyopita mataifa hayo yalipoungana.
"Hatua kubwa zimepigwa kiuchumi, kisiasa na kijamii na hivyo kuna kila sababu ya kujivunia," alisema.
Rais Samia alisema ili kudumisha Muungano kwa miaka ijayo ni vema kuendeleza falsafa ya kuvumiliana, ustahimilivu na kujenga nchi, Kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo endelevu
Alisema Tanzania kwa sasa umepiga hatua kubwa na kufikia uchumi wa Kati ngazi ya chini, akidokeza tathmini zinaonyesha hivi karibuni itafikia uchumi wa kati ngazi ya juu.
Mipaka isitugawe
Akizungumza kuiwakilisha Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Rais wa Burundi, Evarist Ndayishimiye alisema pamoja na wakoloni kuweka mipaka kwa maslahi yao, Tanzania na Burundi zinapswa kuendeleza umoja.
Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, lablaya wakoloni wananchi wa mataifa hayo walishirikiana kibiashara na kijamii.
Alikwenda mbali zaidi na kueleza hata waha na waangaza wa Tanzania hawatofautiani na Warundi kwa mwonekano.
Alieleza wakati huo, Waha wa Uvinza walikuwa wakienda Burundi kuuza chumvi, wakati Warundi wakija Tanzania kuuza majembe.
Kutokana na hayo, alisema ni muhimu kuendeleza uhusiano huo na ndiyo sababu amesafiri kutoka nchini kwake kuhudhuria sherehe hizo.
"Muungano wa Tanzania ni kama Muungano wa Afrika Mashariki, furaha ya Tanzania ni furaha yetu sote kwa sababu sisi ni wamoja," alisema.
Tanzania kinara wa ushirikiano
Akihutubia sherehe hizo kuwakilisha Jumuiya ya Afrika (AU), Rais wa Comoro Azali Assoumani alisema Tanzania inabaki kuwa na sifa ya uahirikiano na mataifa mengi ya Afrika ikiwemo Comoro.
Hilo ni kwa sababu, alisema Tanzania ndiyo kinara wa vuguvugu la kutafuta uhuru wa nchi mbalimbali za Afrika, ikiwemo Comoro.
Mwenyekiti huyo mstaafu wa AU, alisisitiza umuhimu wa nchi hizo kuendeleza ushirikiano kwa maslahi ya maendeleo ya wananchi wa pande zote.
"Viongozi waiotangulia wamejenga msingi ya ukaribu baina ya mataifa mbalimbali na hivyo kuongeza uhusiano, tunapaswa kuendeleza," alisema.
Alitumia jukwaa hilo kuahidi kuendeleza na kudumisha ushirikiano na ukaribu uliopo kati ya viongozi na wananchi wa Comoro na Tanzania, kwa maslahi ya pande zote.
"Mpaka wa Tanzania na Burundi umeletwa na wakoloni na hata sasa ni vigumu kutofautisha Mtanzanía wa Kagera, Kigoma na Warundi," alisema.
Alisisitiza wakati Tanzania unafurahia muungano wake, furaha hiyo ni ya Afrika Mashariki yote kwa ujumla na ndiyo sababu amehudhuria sherehe hizo.
Sherehe zilivyokuwa
Katika sherehe hizo idadi ndogo ya wananchi walishuhudiwa kuhudhuria kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Shughuli hizo zilianza saa 4:16 kwa gwaride na baadaye saa 11:13 viongozi wote walioalikwa walishahudhuria na ratiba kuendelea.
Viongozi waliokuwepo katika sherehe hiyo ni Rais Azali Assoumani (Comoro), Félix Tshisekedi (Jamhuri ya Desmokrasi ya Congo), Évariste Ndayishimiye (Burundi) na Hakainde Hichilema (Zambia).
Wengine ni Hassan Sheikh Mohamud (Jamhuri ya Somalia), William Ruto (Jamhuri ya Kenya) na Nangolo Mbumba (Namibia).
Kwa upande wa Makamu wa Rais waliohudhuria ni Saulos Chilima wa Malawi na Jessica Alupo wa Uganda
Waziri Mkuu wa Msumbiji, Adriano Afonso Maleiane naye ni miongoni mwa viongozi wakuu wa nchi za Afrika waliohudhuria.
Mbali na hao, Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Jenerali mstaafu James Kabarebe na Katibu wa Mambo ya Nje wa chama cha ZANU PF cha Zimbabwe, Balozi Simbarashe Mumbengegwi nao walikuwepo. |
Ni wimbi la majanga lililopoka uhai wa binadamu, kuathiri makazi yao na hata kukwaza shughuli za kiu | Ni wimbi la majanga lililopoka uhai wa binadamu, kuathiri makazi yao na hata kukwaza shughuli za kiuchumi, ndiyo lugha nyepesi unayoweza kuitumia kuakisi kiwango cha athari za mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini.
Mvua hizo za El-Nino zilizoanza kunyesha Oktoba mwaka jana, hadi sasa zimefululiza kwa mwezi wa saba na kukatisha uhai wa watu 160 nchini, kwa mujibu wa taarifa ya Serikali, huku wengine lukuki wakiachwa bila makazi.
Zilianza kwa utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Oktoba mwaka jana, zikitabiriwa kuanza mwezi huo na kutamatika Desemba 2023 na baadaye ilielezwa zitakoma Aprili mwaka huu.
Mvua hizo zinafanishwa na zile zilizonyesha katika kipindi cha kuanzia Oktoba mwaka 1997 hadi Januari mwaka 1998 zilizosababisha vifo vya zaidi ya watu 6,000 katika nchi tano za Afrika Mashariki.
Waliopoteza maisha
Takriban watu 160, wamepoteza maisha kutokana na mvua hizo, kati yao wapo watano waliofariki dunia jana, wilayani Moshi katika Mkoa wa Kilimanjaro na wengine 155 katika mikoa mbalimbali nchini.
Taarifa iliyotolewa jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa iliweka wazi kuhusu idadi hiyo ya waliofariki dunia, huku kaya 51,000 na watu 200,000 wakiathirika.
Athari za mvua hizo, kwa mujibu wa Majaliwa zimezikumbwa zaidi ya nyumba 10,000 nchini, huku nusu ya mikoa ya Tanzania ikikumbwa na athari kwa viwango tofauti.
Mikoa hiyo ni Pwani, Morogoro, Dar es Salaam, Kilimanjaro, Mbeya, Kigoma, Iringa, Tabora, Dodoma, Lindi, Mtwara, Arusha, Kagera, Shinyanga, Geita, Songwe, Rukwa na Manyara.
Familia ilivyopoteza watatu
Katika Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, familia moja imepoteza watoto watatu na watu wazima wengine wawili wamefariki dunia kutokana na mvua hizo.
Hayo yameambatana na majeruhi kadhaa, huku wakazi wengine wa eneo hilo wakiachwa bila makazi, baada ya nyumba zao kuzingirwa na maji na nyingine kusombwa katika Kata za Mji Mpya, Msaranga, Kimochi, Kahe na Mabogini.
Tukio hilo, limetokea usiku wa kuamkia juzi, baada ya Mto Rau kuvunja kingo zake na kusababisha maji yasambae kwenye makazi ya watu.
Akizungumzia hilo, Kaimu Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji, Mkoa wa Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi alisema mmoja kati ya miili iliyoopolea ni wa mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 50 hadi 60.
Kwa upande wa majeruhi, alisema tayari wameshapelekwa katika hospitali kupatiwa huduma.
Nyumba zilivyosombwa
Mvua hizo hazikuiacha salama nyumba ya Marry Agusti, mkazi wa mtaa wa Kwakomba, aliyelalamikia kusombwa kwa nyumba hiyo pamoja na vyakula na mali nyingine.
"Ilikuwa saa tisa usiku, nikasikia mtoto akaniita bibi bibi maji, wakati naitika kugeuka nikakuta maji yamejeaa ndani kila mahali, nilijishika na wajukuu tukaweza kutoka ndani, ambapo wakati huo ukuta katika upande mmoja wa nyumba ulishaanguka huku maji yakizidi kuongezeka," alisema.
Joyce Swai naye amekumbwa na hilo, akieleza hakufanikiwa kuokoa chochote kutoka ndani kwake na sasa amepoteza vitanda, magodoro na vyombo vya ndani.
"Usiku tuligongewa geti kuambiwa mafuriko yanaingia ndani, nilifungua mlango na nilipotoka nikakutana na maji mengi yanaingia, sikuweza kuokoa chochote, niliokoa watoto wangu watatu nikawapeleka eneo lenye muinuko tukawa hapo tukisali hadi saa11 alfajiri ndipo watu wakaja wakavunja ukuta na kutuokoa," alisema.
Upande mmoja wa ukuta wa kanisa la Evangelical International umeondoka na baadhi ya mali vikiwemo viti, kwa mujibu wa mchungaji wa kanisa hilo, Gabriel Shoo.
Kwa ujumla nyumba zilizosombwa na maji pamoja na vilivyokuwa ndani yake ni nne katika Mtaa wa Kwakomba, kama inavyoelezwa na Mwenyekiti wa mtaa huo, Jipson Tesha.
"Katika Mtaa huu, nyumba nne zimeanguka na vitu vyote vilivyokuwa ndani vimesombwa na maji, wananchi wameokolewa ila hawakuweza kuokoa chochote,” alisema.
Nyumba 100 zazingirwa Tegeta
Katika Mkoa wa Dar es Salaam, eneo la Tegeta zaidi ya nyumba 100 zimezingirwa na maji na kusababisha wakazi wake, kuacha mali zilizokuwepo ndani na kuyahama makazi hayo.
Ingawa eneo hilo lina historia ya kukumbwa na mafuriko zinaponyesha mvua, kiwango cha athari kilichotokea sasa ni zaidi ya ilivyotarajiwa.
Pamoja na nyumba za makazi, biashara nazo zilikumbwa na athari hizo za mvua na Corola Antonia mmoja wa wafanyabiasha katika eneo hilo anaeleza undani wa hilo.
Mfanyabiashara huyo aliyekutwa ndani ya maji akiokoa bidhaa zake, alisema kuongezeka kwa mvua ndiko kulikosababisha hali hiyo.
“Mimi ni mfanyabiashara katika eneo hili, kipindi chote nvua ikinyesha maji huwa yanajaa lakini safari hii maji yalikuja kwa haraka kiasi kwamba wengi walishindwa kuokoa mali pamoja na vitu vya ndani,” alisema Antonia.
Nusura Mussa mwenye nyumba iliyozingirwa maji, aliishia kutupa lawama kwa Mbunge wake, Josephati Gwajima (Kawe) kwa kile alichoeleza mwanasiasa huyo ameshindwa kuishinikiza Serikali ifanye maboresho ya miundombinu katika eneo hilo.
Bodaboda kilio
Safari katika baadhi ya maeneo zimekoma kwa madereva wa bodaboda, kutokana na kufungwa kwa barabara kadhaa, lakini sehemu nyingine kuwa na maji mengi.
“Kipindi hiki hatuna kazi kabisa barabara nyingi tunazotumia zimekuwa mashimo tu baada ya kugeuka mifereji, wafanyabiashara tunaowabebea bidhaa zao wamefunga, tunaiomba Serikali kuangalia namna ya kutatua changamoto hii,”alisema Stephan Paulo dereva bodaboda.
Hata hivyo, Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) mkoa wa Dar es Salaam, Geofrey Mkinga alisema tathmini inaendelea kufanyika kubaini kiwango cha athari kwa mkoa wote.
“Kwa sasa hatuwezi kuchukua hatua yoyote kwa kuwa mvua zimenyesha juu ya wastani na ardhi imejaa maji, tunaendelea kufanya tathimini ili kujua madehara kiasi gani na maeneo gani yaliyoathirika zaidi,” alisema Mkinga.
Wabunge wataka hatua
Katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa baada ya kuwasilisha taarifa ya Serikali kuhusu athari za mafuriko bungeni jijini Dodoma, wabunge walisisitiza hatua zaidi kukabili mafuriko.
Pazia la hatua hizo lilifunguliwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Tunza Malapo aliyehoji umuhimu wa mamlaka kutoa taarifa za uwepo wa mvua kubwa ili wanafunzi wasiende shuleni, badala ya kuacha hilo liamuliwe na mzazi.
Katika majibu yake, Majaliwa alisema jukumu la kutoa taarifa za hali ya hewa lipo chini ya kamati za maafa za ngazi za chini ili kuepusha madhara hayo.
“Wakuu wa wilaya na mikoa wajenge utamaduni wa kuwa na mawasiliano na kutoa taarifa wakati wote wanapokuwa na taarifa za hali ya hewa kuwa mbaya katika eneo hilo,” alisema.
Hata hivyo, hatua kuhusu kuwaepusha wanafunzi na athari za mafuriko, zilielezwa juzi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda aliyezitaka shule kuchukua hatua za tahadhari.
Alisema wazazi wana haki ya kutoruhusu watoto kwenda shule endapo watakuwa na wasiwasi na hali ya hewa ya siku husika.
Hoja nyingine bungeni hapo, iliibuliwa na Innocent Kalogeresi, Mbunge wa Morogoro Kusini, aliyehoji mpango wa Serikali kukabiliana na mafuriko mkoani Morogoro, akiiambatanisha na mkakati wa kuchimba mabwawa ili kupunguza kasi ya mito.
Akijibu hilo, Majaliwa alisema tayari wataalamu wa Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi wapo maeneo sahihi ya kuangalia panakopaswa kuchimbwa mabwawa.
“Tayari wataalamu wako huko kuona maeneo sahihi ya kuchimba ili kuchepusha maji kutoka kwenye mfereji mkubwa wa Rufiji kupeleka kwenye mabwawa. Mkakati huo unaendelea mpaka uelekeo wa Mto Wami kupitia mfereji huo wanachimba bwawa la Kidunda kwa ajili ya matumizi ya maji ambayo yataingia Dar es Salaam,” alisema.
Alisema tayari fedha zimeshatengwa kwa ajili ya kuchimba mabwawa Rufiji na mengine yataendelea kuchimbwa katika bonde la Ruvuma na Nyasa na kwamba fedha za shughuli hiyo zitaongezwa kwa kadri zitakavyopatikana.
Mabwawa nchi nzima
Pamoja na mabwawa aliyoeleza Majaliwa, Aprili 12, mwaka huu Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi alisema Serikali inatarajia kuchimba jumla ya mabwawa Katika mkutano na waandishi wa habari, Msemaji Mkuu wa Serikali, Matinyi alisema Serikali inatarajia kujenga mabwawa mawili wilayani Rufiji ikiwa ni hatua za muda mrefu za kukabiliana na athari za mafuriko katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa Matinyi, mabwawa hayo mawili yanayojengwa Rufiji ni kati ya 127 ambayo Serikali inatarajia kuyajenga katika mikoa mbalimbali nchini na tayari upembuzi yakinifu umeshafanyika.
Alisema mengine 14 ujenzi wake umeshaanza katika maeneo kadhaa nchini.
"Aprili 20, 2024 Serikali itatangaza zabuni ili kumpata mkandarasi atakayejenga mabwawa hayo 127," alisema Matinyi.
Maelekezo 14
Majaliwa alitumia jukwaa la bunge, kutoa maelekezo 14 kukabiliana na maafa ya mafuriko, ikiwemo kushirikiana na wadau kutekeleza majukumu yaliyoanishwa katika Mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na Madhara ya El-Nino.
Mengine ni kamati za maafa za mikoa zitoe tahadhari kwa wananchi, wananchi wafuatilie taarifa za utabiri wa hali ya hewa, wakuu wa mikoa na viongozi wa chini yao wasimamie usafi wa maeneo yao.
Pia, alielekeza viongozi washirikiane kudhibiti uharibifu wa mazingira, halmashauri na wamiliki wa shule binafsi waweke utaratibu wa kufidia masomo kwa shule zitakazofungwa, madereva wa magari ya shule wajiridhishe na njia wanazopita na wazazi wahakikishe kuangalia usalama wa wanafunzi.
Maelekezo mengine ni Tanroads na Tarura, Tazara na TRC zifanye tathmini ya barabara na njia za reli zilizoathirika na mafuriko na kuweka mpango wa kukarabati haraka ili kurejesha mawasiliano.
Aidha, alitaka wabainishe maeneo yanayopitiwa na mikondo ya maji kote na kuweka alama za tahadhari.
Pia, alilielekeza Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani litoe tahadhari kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara, Kamati za Maafa Vijiji, Wilaya na Mikoa zisimamie ugawaji wa misaada inayotolewa kwa waathirika.
Maelekezo mengine ni Viongozi wa Serikali ngazi zote wahamasishe na kuelimisha wananchi wanaoishi mabondeni kuhamia maeneo salama, mamlaka za mipango miji zisimamie kikamilifu mipango miji ya Halmashauri na kudhibiti ujenzi holela unaozuia njia za maji.
Pia, alielekeza Wizara ya Afya itoe elimu ya afya ya jamii ili kudhibiti magonjwa ya mlipuko na kuhakikisha upatikanaji wa tiba.
Mbinu za kitaalamu
Uwepo wa utashi wa kisiasa, matumizi ya sayansi kupewa nafasi na kubainishwa kwa maeneo hatarishi ni miongoni mwa hatua zilizopendekezwa na wanazuoni kukabiliana na athari za mafuriko nchini.
Katika maelezo yake, mtaalamu wa majanga wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Egidius Kamanyi alisema utashi wa kisiasa ndiyo utakaoifanya Serikali ione umuhimu wa kujali na kulinda watu wake dhidi ya majanga.
“Utashi ndiyo utakaozalisha sababu ya kuanzisha mchakato wa kutafuta suluhu au namna ya kukabiliana na majanga kwa mbinu za kisayansi,” alisema Dk Kamanyi.
Aliambatanisha hoja yake hiyo na msisitizo wa sayansi kupewa nafasi katika kukabili majanga hayo ya mafuriko.
“Tuchukulie mfano kwenye miji yetu, ujenzi umefanyika bila mpangilio, baadhi wamefuata vyanzo vya maji na hawakuzingatia mbinu za kisayansi. Bado Serikali inaendelea kuruhusu ujenzi holela,” alisema.
Kuipa nafasi sayansi, alieleza ni hatua ya kutoruhusu uendelezwaji wa eneo lolote bila kufanyika upembuzi yakinifu na utafiti wa kisayansi ili kufanya makisio ya athari zinazotarajiwa.
Mbinu kuwang’oa wa bondeni
Mwanazuoni huyo aliyebobea katika taaluma ya udhibiti wa majanga, alisema mara nyingi Serikali inachukua hatua ya kutaka kuwahamisha wananchi kutoka maeneo hatarishi, lakini haifanikiwi.
Pamoja na kushindikana huko, Dk Kamanyi alisema hakujafanyika tathimini ya kujua kwa nini watu wanaoishi mabondeni au maeneo hatarishi kwa mafuriko wanagoma kuhama wanapoamrishwa na Serikali.
Jawabu la hilo linatokana na utafiti uliowahi kufanywa na Dk Kamanyi na kubaini wengi wanagoma kuhama kwa hofu ya kutenganishwa na watu waliowazoea.
“Nilibaini watu wengi kwenye maeneo hayo wanaishi kindugu. Akiwa hana kitu ataenda kwa jirani ataomba atapewa, akikosa fedha ataenda kwa jirani atapewa chakula atakula, sasa huyu unapotaka kumhamisha anawaza hivi kwa maisha yangu nitaishije,” alieleza.
Sababu nyingine alieleza ni ukaribu na maeneo ya utafutaji, mathalani wakazi wa Jangwani, jijini Dar es Salaam.
“Mtu anakaa Jangwani anajua asubuhi anaenda Kariakoo kwa mguu, anasukuma mkokoteni anapata chochote anarudi kwa mguu nyumbani, familia inapata chakula. Ukimpeleka Mabwepande hatakuelewa, atafikaje Kariakoo?” alihoji Dk Kamanyi.
Uhamishaji wananchi kutoka eneo moja kwenda lingine, Dk Kamanyi alisema unapaswa kuhusisha kuwekwa kwa miundombinu itakayowashawishi na kuwawezesha kuishi ama kama walivyokuwa wanaishi awali au zaidi.
Dk Kamanyi alisisitiza pendekezo lake hilo kwa hoja kuwa, uhamishaji wananchi haupaswi kugubikwa na ahadi hewa bila utekelezaji na kwamba, ndicho kinachofanywa na Serikali.
“Siyo unawapeleka eneo fulani unawatelekeza, Serikali inapaswa kuandaa miundombinu na mazingira yatakayowawezesha kuishi vizuri katika makazi mapya,” alisema Dk Kamanyi.
Miongoni mwa maandalizi anayosema ni muhimu kufanywa kabla ya kuwahamisha wananchi ni ujenzi wa maeneo ya kupata huduma muhimu zikiwamo za afya, elimu, maji, malazi na uchumi.
Alisema hayo yaambatane na kuwajengea barabara na kuruhusu daladala kufanya safari za kwenda kwenye eneo kama hilo ili kurahisisha usafishaji.
Yote hayo alisema yasifanyike kabla ya kuwauliza wananchi wenyewe, waeleze mazingira ambayo wangetamani kuishi kwa utulivu, kisha washawishiwe kulingana na uwezo wa Serikali.
Mtazamo huo unashabihiana na kilichoelezwa na Dk Enock Makupa, mtaalamu wa udhibiti wa majanga wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), anayesema utaratibu unaotumika kuwahamisha wananchi ndiyo unaofanya wakubali au wakatae.
Utaratibu sahihi, Dk Makupa anasema unapaswa kuanza kwa kutoa elimu jambo ambalo aghalabu hufanyika, kisha kuwaonyesha makazi mbadala, akifafanua hapo ndipo lilipo tatizo.
“Unakuja Serikali inamfuata mwananchi ikimtaka kuhama kutoka eneo moja kwenda lingine, inamwambia utahamia sehemu fulani nitakupa mabati na tofali, unapomuhamisha umemkuta ameshajenga nyumba, unatarajia atakubali kuhama?” amehoji Dk Makupa.
Anasisitiza tatizo la wananchi kugoma kuhama mabondeni halipo kwao, bali taratibu zinazotumika na Serikali kuwahamisha ndilo tatizo.
“Serikali inapaswa kuandaa eneo na kuweka miundombinu yote muhimu ndipo iende kushawishi wananchi kuhama, huku ikiwaonyesha kwamba mtahamia hapa,” anaeleza Dk Makupa.
Mwanazuoni huyo anaeleza kunahitajika wataalamu kwa ajili ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu majanga kama hayo, lakini bado hawatumiki kwa kazi hiyo.
“Mara nyingi tunaona yakitokea majanga Serikali inaunda kamati za Bunge, huko wanaenda kutembelea ilhali hawana utaalamu wanaishia kufanya mambo kisiasa, kesho hali inajirudia,” anasema.
Maeneo hatarishi yabainishwe
Kwa mtazamo wa Dk Makupa, ili kupunguza athari za mafuriko ni muhimu Serikali iyabaini maeneo hatarishi kwa janga hilo na yawekwe alama ili wananchi wasiruhusiwe kuishi.
“Tukifanya hivyo, mafuriko yakitokea tunapunguza madhara kwa wananchi na mali zao, kwa kuwa hawataishi tena kwenye maeneo hatari, hivyo watakuwa salama,” anasema.
Jambo lingine linalopaswa kufanyika kwa mujibu wa Dk Makupa, ni utolewaji wa elimu kwa wananchi juu ya majanga ya asili na namna ya kuyaepuka.
Hata hivyo, mwanazuoni huyo anaeleza kuwapo changamoto katika mfumo wa utendaji wa kamati za maafa kuanzia ngazi ya Taifa hadi vijiji.
Anasema kamati hizo ndizo zenye jukumu la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majanga, lakini mara nyingi zilizopo ngazi ya vijiji hazijui zifanye nini. |
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimesema 2023 ni mwaka ambao uzingatiwaji wa haki za bi | Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimesema 2023 ni mwaka ambao uzingatiwaji wa haki za binadamu ulidorora ukilinganisha na mwaka 2022.
Msingi wa tathmini hiyo ya LHRC, ni utafiti wa haki za binadamu wa mwaka 2023 ilioufanya katika mikoa 20 ya Tanzania bara na mikoa yote ya Zanzibar.
Hali hiyo kwa mujibu wa ripoti ya utafiti huo, ilichagizwa na kuendelea kwa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwemo ukatili dhidi ya wanaume, wazee, watoto, wanawake na watu wenye ulemavu.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mwaka 2023 haki ya kuishi, uhuru dhidi ya vurugu, haki ya usawa mbele ya sheria na haki ya uhuru na usalama binafsi ndizo haki za binadamu zilizokiukwa zaidi, huku mikoa saba ikiwa vinara kwa ukiukwaji huo..
Ukatili
Katika ripoti hiyo vitendo vya ukatili dhidi ya wanaume vimeongezeka na kufikia asilimia 10 mwaka 2023 kutoka asilimia sita ya mwaka 2022.
Wazee nao walikatiliwa zaidi mwaka jana hadi kufikia asilimia 12, kutoka asilimia 10 ya mwaka 2022 kwa mujibu wa ripoti hiyo.
Hali imebaki kuwa mbaya kwa ukatili dhidi ya watoto ambao ni asilimia 45, ukipungua kutoka asilimia 47 ya mwaka 22, huku wanawake wakifikia asilimia 30 kutoka 33 ya mwaka 2022.
Ripoti hiyo inaeleza watu wenye ulemavu waliokumbana na ukatili mwaka 2023 ni asilimia tatu, kutoka asilimia nne ya mwaka 2022.
Hata hivyo, ripoti hiyo inaweka wazi kuwa haki ya kuishi iliendelea kukiukwa mwaka 2023 kutokana na vitendo mbalimbali ikiwemo mauwaji ya watu wasio na hatia, hukumu za vifo, ajali za barabarani, mauwaji ya wenza na kutoweka.
“LHRC ilirekodi matukio 42 ya unyanyasaji wa makundi, ambayo ni mawili zaidi ya yale yaliyorekodiwa mwaka 2022,” inaeleza sehemu ya ripoti hiyo.
Kadhalika, ripoti hiyo inabainisha huku 37 za vifo zilitolewa na mahakama kuu nchini, kati ya hizo wanaume ni asilimia 94, jambo linaloonyesha kuendelea kwa hukumu hizo.
Kwa upande wa mauwaji ya wenza, ripoti hiyo imetaja matukio 50 ya wenza waliouwana, ikiwa ni 17 zaidi ya yaliyoripotiwa mwaka 2022.
Katika matukio hayo ya mwaka 2023, kwa mujibu wa ripoti hiyo, asilimia 90 ya wahanga ni wanawake na wanaume ni asilimia 10 .
“Bado mwaka 2023 hakukuwa na majibu kutoka mamlaka mbalimbali za Serikali juu ya watu waliopotea kwa miaka saba iliyopita, akiwemo mwandishi wa habari, Azory Gwanda,” inaeleza sehemu ya ripoti hiyo.
Licha ya juhudi zilizofanywa katika kupunguza ajali za barabara, ripoti hiyo inabainisha zaidi ya watu 500 wanaendelea kupoteza maisha kila mwaka kwa ajali hizo.
Mara nyingi matukio hayo huchagizwa na mwendokasi, ulevi wakati wa kuendesha, kufeli kwa breki na mambo mengine.
Uhuru wa kujieleza nao, umeendelea kuwa tatizo kwa mujibu wa ripoti hiyo, ikielezwa matukio mawili yaliripotiwa katika Mkoa wa Dar es Salaam na Arusha.
“Pamoja na wanahabari kuwa na furaha na mwenendo wa uongozi wa vyombo vya habari, wamesisitiza kwamba ni vigumu kupata uhuru kamili bila mabadiliko ya kisheria,” inaeleza ripoti hiyo.
Usawa mbele ya sheria
Asilimia 78 ya wananchi waliofikiwa katika utafiti huo, wameeleza rushwa ndicho kikwazo kikubwa cha kupata haki, huku asilimia 49 wakitaja kesi kukaa muda mrefu, asilimia 48 wametaja uelewa mdogo wa sheria na asilimia 39 ni gharama za kupata uwakilishi mahakamani.
Bado mamlaka za haki jinai zimetajwa kutumia nguvu zaidi zinapomuhitaji mtuhumiwa, huku rushwa nayo ikiendelea kuwa mwiba.
Matukio ya kujichukulia sheria mkononi yaliongezeka kwa Julai 2022 hadi Mei 2023, yalifikia 45,455.
“Wivu, imani za kishirikina, mirathi hasa ya ardhi ndizo sababu za hatua hizo,” alieleza ripoti hiyo.
Matukio ya vitisho pia, yaliongezeka mwaka 2023 na kufikia 57, kutoka 44 ya mwaka 2022.
Ripoti hiyo, nimebaini upungufu wa asilimia 50 ya wafanyakazi katika sekta ya afya na hata bajeti katika sekta hiyo bado haijafikia viwango stahiki, licha ya kuongezeka kwa asilimia 15.
Katika utafiti huo, asilimia 39 ya wazee wamelalamikia hatua ya watoto wao kuwaachia mzigo wa kuwalea wajukuu.
Mapendekezo
Kutokana na yote yaliyobainika, LHRC inapendekeza maboresho ya kisera na kisheria katika mifumo ya haki jinai na mabadiliko ya Katiba.
Akizungumzia ripoti hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga alisema jambo zuri ndani ya utafiti huo kwa mwaka 2023 hakuna tukio la mauwaji ya albino lililobainika.
Pamoja na hali hiyo, alisema ni muhimu elimu ikaendelea kutolewa kwa kuwa matukio hayo mara nyingi hutokea katika kipindi ambacho uchaguzi unakaribia.
“Kwa sababu tunakaribia uchaguzi hatuna budi kutoa elimu, maana kipindi kama hiki ndipo matukio ya mauaji ya albino hutokea, wapo watu wanaodhani ushindi wa uchaguzi unatokana na uhai wa mtu,” alisisitiza.
Mtafiti Mwandamizi wa LHRC aliyesimamia utafiti huo, Fundikira Wazambi alisema matukio yaliyobainishwa yana athari kwa watu binafsi na uchumi wa nchi.
Alisema kuendelea kutokea kwa matukio hayo, kunasababishwa na kukosekana kwa uwajibikaji katika ngazi zote.
"Wapo wanaoshuhudia matukio lakini hawataki au wanaogopa kuripoti katika Mamlaka zinazohusika, mimi nimewahi kushuhudia kiongozi anaogopa kuripoti," alisema.
Rushwa nayo ni sababu nyingine ya kuendelea kwa vitendo hivyo, kwa mujibu wa Fundikira.
Alisema wapo wanaofanya matukio hayo kisha wakawahonga wazazi wa muathirika ili akafute kesi mahakamani. |
Kamati ya Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana imemuhoji kwa takribani saa tatu Mkuu wa Mkoa wa | Kamati ya Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana imemuhoji kwa takribani saa tatu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda.
Makonda ambaye Aprili 16, mwaka huu, alitumiwa barua ya wito ikimtaka kufika mbele ya kamati hiyo Aprili 20, mwaka huu, lakini jana Aprili 22, 2024 ndio .amefika mbele ya kamati hiyo kwa mahojiano.
Mwananchi ambalo jana liliweka kambi kwenye ofisi za Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma, lilimshuhudia Makonda akiingia kwenye ofisi hizo saa 3:15 asubuhi akiwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser rangi ya kijivu.
Awali, haikufahamika wito wa Makonda mbele ya kamati hiyo huku ikihisiwa kwamba, huenda ni kauli yake aliyoitoa kwenye kumbukumbu ya miaka 40 ya kifo cha Waziri Mkuu wa zamani, Hayati Edward Sokoine.
Kwenye maadhimisho hayo, Makonda aliposimama kusalimia alidai kuna baadhi ya viongozi wa Serikali wakiwemo mawaziri wamekuwa wakilipa watu ili kumtukana Rais Samia Suluhu Hassan mwenye mitandao ya kijamii.
“Kuna watu wanahusika na kumchafua Rais Samia kwenye mitandao ya kijamii. Nitumie fursa hii kuwaambia hasa kaka zangu, mnaotuma na kuwalipa watu kumchokoza mama yangu, ninawajua na ninyi mnawajua. Narudia tena hasa kaka zangu mnaotuma kulipa watu kumchokoza mama yangu Samia.
“Nawajua kwa majina na leo tarehe 12 (Aprili 12, 2024), nataka iwe mwisho kuwatuma watu kwenye mitandao ya kijamii kumtuka Rais Samia na Jumatatu (Aprili 15, 2024) ikiendelea natataja majina, wengine ni mawaziri,” alisema Makonda na kuongeza: “Naomba kukutia moyo, mimi nina mtoto wa kike na najua wengi wana watoto wa kike, wanatamani watoto wao wa kike, ikiwemo na mimi waje wasome hadithi njema za uongozi uliofanywa na kiongozi mwanamke na mahiri ambaye anaongoza Taifa hili.
“Ulinzi wa bunduki na watu wa usalama kwa taarifa unaweza usiuponye moyo, lakini neno la uzima linalotoka kwa watumishi wa Mungu linaweza kuponya moyo wako, nakuombea kwa Mwenyezi Mungu, akupe wigo na utakaolinda moyo wako, ili ututumikie sisi Watanzania.”.
Habari za kuaminika kutoka vyanzo vyetu zimeeleza kuwa, Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara, Abdulrahman Kinana ndiye aliyeongoza mahojiano hayo ya Makonda akiwa na wajumbe wengine watano.
Imeelezwa kuwa Makonda amehojiwa kuhusu tuhuma hizo alizozitoa kuwa kuna viongozi wakiwemo mawaziri wamekuwa wakimchafua Rais Samia kupitia mitandao ya kijamii kwa kuwalipa watu kufanya kazi hiyo.
Chanzo hicho kimeeleza kuwa wajumbe wa kamati hiyo walimtaka Makonda kuwataja viongozi wakiwemo mawaziri ambao, amewatuhumu kuhusika na matendo hayo.
“Ni kweli leo (jana) asubuhi Makonda alifika hapa ofisini kwa ajili ya kuitikia wito wa kamati ya maadili. Kikao kiliketi kwa takribani saa tatu na kilikuwa cha kawaida.
“Mahojiano yalikuwa ya kawaida lakini, kubwa Makonda alitakiwa kuwataja watu aliosema anawafahamu kwa majina kuhusika katika kumchafua Rais Samia ili Chama kichukue hatua stahiki,” kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo, chanzo kingine kilidai kuwa Makonda hakuwa tayari kutaja majina ya wahusika akieleza kuwa, chama na Serikali kina vyombo vyenye uwezo wa kuchunguza hivyo, wanaweza kuvitumia kupata ukweli.
Chanzo hicho kimedai kuwa Makonda aliamini chama hicho kilipaswa kufungua jalada la uchunguzi na kuwaalika watu wenye taarifa kuhusu madai aliyoyatoa badala ya kumtaka yeye awataje.
“Nilimuona Makonda hapa leo (jana) kwa ajili ya kuhojiwa na kamati yam zee Kinana. Ila ninachofahamu ni kuwa alitakiwa kuwataja watu aliodai anawafahamu kwa majina, lakini amegoma akitaka chama kitimize wajibu wake kwa kutumia vyake ili kupata ukweli. Kwa hiyo jamaa kagoma kuwataja majina, sijajua sasa kikao kitaamua kitu gani,” kilisema chanzo chetu kingine.
Kauli yake ilivyogawa makundi
Makonda ambaye kabla ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha alikuwa akihudumu kama Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo aliyodumu kwa miezi mitano.
Uteuzi wake kuwa mkuu wa mkoa ulihusisha na kauli yake aliyoitoa wakati wa mapokezi ya ndege ya Shrika la Ndege la Tanzania (ATL) aina ya Boeing 737-Max 9 ambako Makonda aliwashukia viongozi akisema ni unafiki kumtofautisha Rais Samia na mtangulizi wake Dk John Magufuli.
Tangu wakati huo kumekuwa na mitazamo tofauti kuhusu kauli za Makonda huku wachambuzi wa siasa wakidai kuwa kuna vita kubwa ndani ya CCM ikihusishwa na makundi ya urais.
Uhalali wa CCM kumhoji Makonda
Ni halali kwa kamati ya maadili ya chama hicho kumhoji Makonda, bila kujali wadhifa wake ndani ya Serikali kutoshabihiana na uongozi wa CCM.
Kinachohalalisha hilo ni uanachama wake wa CCM ambao kwa mujibu wa Kanuni ya Usalama na Maadili ya chama hicho, kamati hiyo ina haki na wajibu wa kumhoji mwanachama yeyote iwapo atakiuka maadili.
Hata hivyo, kanuni hiyo inaeleza kuhusu tuhuma lakini haijamwelezea mtuhumu. Isipokuwa imetaja kitendo cha unafiki na kuvuruga amani ndani ya chama kama miongoni mwa makosa ya kimaadili.
Kwa kosa kama hilo, adhabu iliyotajwa kwa mujibu wa kanuni hiyo ni onyo la karipio na itakapoonekana mkosaji hajirekebishi licha ya kuadhibiwa ataadhibiwa zaidi, ikiwemo kufutiwa uanachama wake.
Kosa kubwa zaidi ya yote linalotajwa ndani ya kanuni hiyo ni kukisaliti chama hicho, ambalo adhabu yake moja kwa moja ni kufukuzwa uanachama na aghalabu hutangazwa hadharani.
Mtazamo wa wadau
Hata hivyo, hatua ya Makonda kuitwa na mamlaka hiyo ya nidhamu ya chama chake, ilitarajiwa kwa kile alichokifanya, kama inavyoelezwa na Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Profesa Mohamed Bakary.
Profesa Bakary alisema tuhuma zake dhidi ya mawaziri ni jambo baya na hakupaswa kutumia jukwaa alilolitumia kuyaeleza aliyoyaeleza.
Kitendo cha Makonda kueleza hayo mbele ya umma kimechafua taswira ya Serikali kuwa kuna mikwaruzo ndani yake, ilhali wakati wote inapaswa kuonekana ni moja.
“Ni kauli mbaya na inaonyesha hakuwa na umakini katika kuongea katika majukwaa labda kama ilikuwa na nia ya kujipatia sifa mbele ya aliyemteuwa,” alisema Profesa Bakary.
Kwa mujibu wa Profesa Bakary, kwa kauli hiyo lazima angeitwa na mamlaka ya nidhamu kupitia chama chake au Serikali ili ahojiwe na aeleze.
Mwanazuoni huyo alisisitiza hata kama Makonda ana ushahidi dhidi ya alichokizungumza bado kitendo cha kueleza hadharani ni kosa.
Waliowahi kuhojiwa
Makonda si kiongozi wa kwanza kuhojiwa na kamati hiyo, wapo vigogo kadhaa waliowahi kupitia hayo, akiwemo Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara wa sasa, Abdulrahman Kinana.
Kinana walihojiwa pamoja na Katibu Mkuu wa zamani wa chama hicho, Yusuph Makamba kwa tuhuma za utovu wa nidhamu na Kinana alikaripiwa, huku Makamba akionywa.
Si hao tu, Sophia Simba akiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Taifa (UWT), alikumbana na mahojiano na kamati ya maadili yaliyohitimishwa na uamuzi wa kufukuzwa kwake.
Sophia alifukuzwa CCM na wenzake akiwemo Wenyeviti wa zamani wa CCM wa Mikoa ya Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, Iringa Jesca Msambatavangu, Shinyanga Erasto Kwilasa na Mara Christopher Sanya kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho. |
Ili kudhibiti upotevu wa mali na mapato yake, Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) limeanzisha mifu | Ili kudhibiti upotevu wa mali na mapato yake, Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) limeanzisha mifumo ya kidigitali kwa ajili ya kuratibu shughuli zake.
Kabla ya matumizi ya mifumo hiyo, Baraza hilo lilikabiliwa na changamoto lukuki katika urasimishaji wa rasilimali zake na wakati mwingine kushindwa kudhibiti ubadhilifu.
Hayo yalielezwa jana na Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir alipozungumza na Mwananchi kuhusu mabadiliko ya mifumo hiyo.
Alisema kupitia mifumo hiyo kwa sasa Bakwata itarasimisha rasilimali zake, fedha, misikiti, viongozi, miradi, walimu wa madrasa, madrasa na wachinjaji wote.
Kwa mujibu wa Mufti huyo, hilo litafanyika kwa vitu hivyo kusajiliwa kwenye mfumo maalum wa programu tumizi ya baraza hilo itakayoitwa Bakwata App.
"Bakwata kwa sasa tumeamua kuiwekea mifumo ya kidigitali na muda so mrefu itaanza kutumia namba maalum ya kukusanya mapato kwa kutumia mifumo yake ya Kisasa," alieleza.
Pamoja na mambo mengine, alieleza msingi wa mabadiliko hayo ni kuhakikisha baraza hilo linatimiza madhumuni ya kuanzishwa kwake.
Alisisitiza linafanyika hilo, kwa kuwa baraza hilo lina mipango ya maendeleo na huduma kwa jamii kupitia miradi ya Vituo vya Afya, Zahanati na mingine ya kiuchumi.
"Jambo linaloendelea ni kuwajengea uwezo viongozi wote wa Bakwata kuanzia misikiti hadi Mikoa kwa kuwapa mafunzo ya uongozi, Tehama, ujasiriamali na maarifa mengine muhimu ya kuandaa mipango na ufuatiliaji," alisema.
Mufti huyo alisema hata mafunzo hayo, yatatolewa kwa njia ya kidigitali kupitia Bakwata online Academy.
Akizungumzia hayo, Imamu wa Msikiti wa Tunungua mkoani Morogoro, Said Ng’atsegwa alisema hayo ndiyo mambo yaliyosababisha Mufti hiyo atunukiwe Shahada ya Udaktari wa Heshima kutoka Chuo Kikuu Huria cha Gambia.
"Amekuwa na maono makubwa yanayofanya Bakwata tuende kuwa na udhibiti thabiti wa mali zetu. Shahada aliyotunukiwa ni halali yake mwenye macho na akili haambiwi tazama," alisema.
Pamoja na hayo, alisema Mufti huyo ameanzisha Tuzo za Kitaaluma zinazotolewa kwa wanafunzi waliofanya vizuri kwenye masomo mbalimbali hasa hesabu na Sayansi bila kubagua dini.
"Mwaka jana alitoa tuzo kwa kijana wa kidato cha sita wa Marian boys kwa jina John Wilbald aliyeongoza kitaifa katika masomo ya Fizikia, Kemia na Hisabati kwa kiswahili sahihi Tahsusi ya PCM," alisema. |
Safari ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imefikisha miongo sita, umri ambao unatajwa kuwa mrefu | Safari ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imefikisha miongo sita, umri ambao unatajwa kuwa mrefu zaidi kati ya miungano yote iliyowahi kutokea katika bara la Afrika.
Mataifa hayo yaliungana Aprili 26, 1964 chini ya waasisi wake, Mwalimu Julius Nyerere kwa Tanganyika na Abeid Amani Karume kwa upande wa Zanzibar.
Unaweza kuwa miongoni mwa miungano inayopaswa kupigiwa mfano, kutokana na umri wake, kadhalika uimara ulionao, ingawa zipo changamoto zinazotajwa kuuhusu.
Kinachofanya muungano huo uingie katika historia ya kupigiwa mfano ni ukweli kwamba, yapo mataifa ya Afrika yaliyothubutu kuungana na hatimaye hayakudumu katika umoja huo.
Miongoni mwa mataifa hayo ni Ghana na Guinea baada ya mkutano wa watu wa Afrika na mwaka 1959, muungano huo ulitangazwa kuwa utatambulika kama Umoja wa Dola za Kiafrika.
Mambo yalinoga zaidi mwaka 1961, taifa la Mali lilipojiunga na umoja huo na kuufanya uwe na mataifa matatu. Lakini furaha hiyo ilidumu kwa mwaka mmoja baada ya 1962, muungano huo kuvunjika kutokana na vita baridi.
Senegal na Gambia nazo ziliungana mwaka 1981 na kuunda Senegambia iliyodumu hadi mwaka 1989 kisha kuvunjika.
Hiyo ni michache kati ya mifano mingi ya mataifa ya Afrika yaliyoungana lakini hayakudumu maisha ya muungano, tofauti na ilivyo Tanganyika na Zanzibar.
Ukiacha ukongwe wake, ipo minong’ono kuuhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar, jambo ambalo kuna wakati linagawa mitazamo ya Watanzania.
Msimamo wa ACT
Upo upande unaoona si vema kuzungumzia changamoto zilizopo ndani ya muungano kwa dhana kuwa, kunahatarisha uhai wake, lakini wapo wale unaodhani ni haki kero zizungumzwe na huu ndiyo msimamo wa Chama cha ACT Wazalendo.
Katika mahojiano maalum na gazeti hili, Kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu anasema kiu yake ni kuwepo kwa muungano imara, wa haki sawa na kuheshimiana.
Katika kuyafikia hayo, mwanasiasa huyo anaona ni muhimu kero zinazolalamikiwa zijadiliwe na kutafutiwa ufumbuzi.
“Tukiwa na fursa ya kujadili muungano, ndivyo tutakuwa na muungano bora zaidi. Kwa hiyo sisi tunajiona kama chama ambacho tutaleta mawazo chanya kwenye muungano na kuruhusu uhojiwe,” anasema.
Kwa mujibu wa Dorothy, kufanya hivyo kutawezesha wananchi wa pande zote washiriki katika kuuboresha muungano ambao kimsingi unagusa maslahi ya wote.
Kiongozi huyo anapingana na mitazamo kuwa, kuujadili na kuuhoji muungano ni chachu ya kuvunjika kwake, akifafanua ni vema watu wauzungumze ili kuuimarisha.
“Sio kwamba sisi hatuutaki muungano, tunautaka lakini tumeeleza tunataka wa aina gani. Pia muungano huu hata wazee wetu walikaa chini wakajadili na sasa miaka 60 imepita kuna mawazo mapya, kuna mifano mingi tunayoweza kuiga ili uwe na manuaa kwa wote,” anasisitiza.
Anaeleza si suala jema kuwa na muungano ambao upande mmoja unalalamika kunyonywa.
Anatoa msimamo wa chama hicho ni muungano wa Serikali tatu, ambazo ni Tanganyika, Zanzibar na ile ya Muungano na kwamba kitasimamia utekelezwaji wa hilo.
“Tutaendelea kusimamia hayo kwa lengo la kuboresha muungano na si vinginevyo,” anaeleza.
Miaka 60 ijayo ya muungano
Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, Issihaka Mchinjita anasema taswira ya miaka 60 ijayo ya muungano itategemea mambo yatakayofanyika kuweka misingi mizuri ya kuondoa changamoto.
Kwa mtazamo wa Mchinjita, changamoto ya muungano ni muundo wake na kwamba mabadiliko ya Katiba yanaweza kuwa dawa yake.
“Ni muungano unaounganisha nchi mbili lakini baada ya kuunganisha nchi moja inayoonekana nchi moja haionekani na nchi isiyoonekana inakuja kuwa ndiyo huo muungano,” anasema.
Kwa namna muungano huo ulivyo, anasema hata kukiwa na tatizo hatakuwepo wa kujadiliana naye, badala yake mjadala utakuwa kati ya nchi na muungano wenyewe.
Anaeleza iwapo hayo yatafanyika baada ya miaka 60, Tanzania itakuwa ni nchi ya muungano wenye heshima, utakaozaa fursa za kimuungano na hautominya upande wowote.
“Tukifanya hivyo tutakuwa na muungano ambao rasilimali za taifa zitatumika vema na kutoa mchango bora kwenye huo muungano,” anasema.
Anaeleza Zanzibar ikiwa taifa lenye uwezo wa kutumia fursa ilizonazo kuwanufaisha wananchi wake na zikawa na maslahi kwa mataifa yote hapo ndipo muungano utakuwa na tija.
Anasisitiza muungano utakuwa imara iwapo nchi itakubalika kujadiliwa kwa mambo yote yanayoonekana ni kero za muungano.
“Haya mambo yamo kwenye mfumo wenyewe wa muungano,” anaeleza.
Chama cha ACT Wazalendo ni moja ya vyama vinavyounda Serikali ya Zanzibar pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Kuingia kwake ndani ya Serikali hiyo kulitokana na matakwa ya kisheria yanayoipa nafasi ya kuwa sehemu ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa baada ya kuwa katika nafasi ya pili katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.
Kwa sasa chama hicho, kimetoa Makamu wa Kwanza wa Rais, Othman Masoud aliyerithi nafasi ya Maalim Seif Sharif Hamad ambaye Februari mwaka 2021, alifariki dunia.
Chama hicho kinakuwa cha pili kuunda SUK, ambayo awali iliundwa na CCM na Chama cha Wananchi CUF na Maalim Seif ndiye aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais. |
Ni mkakati wa wagombea au ni mapenzi ya wanachama? Ndilo swali unaloweza kuuliza kutokana na kinacho | Ni mkakati wa wagombea au ni mapenzi ya wanachama? Ndilo swali unaloweza kuuliza kutokana na kinachoendelea katika uchaguzi wa kuwapata viongozi wa kanda wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Katika mchakato huo, imeonekana harufu ya ushindani mkali kuelekea uchaguzi huo wa Mei, mwaka huu baada ya sehemu kubwa ya wagombea kutoshana nguvu katika harakati za kuchukua fomu.
Ukiachana na Mchungaji Peter Msingwa na Ezekiah Wenje ambao makundi ya wafuasi wao ndiyo yaliyowachukulia fomu za kuwania nafasi hizo, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ naye amefuata mwendo huo.
Pengine Msingwa na Wenje ndiyo walioonekana kuwa na ushawishi zaidi baada ya kuchukuliwa fomu na wafuasi wao, lakini hatua ya Sugu kuingia kwenye njia hiyo, kunaongeza ugumu wa kujua nani anayenukia kutwaa nyadhifa hizo.
Waliofungua pazia la kumchukulia mgombea fomu ni wanachama 50 kutoka Mikoa ya Mwanza na Geita, waliojitokeza kumchukulia Wenje katika ofisi za kanda hiyo zilizopo jijini Mwanza.
Hilo liliratibiwa na mmoja wa wanachama hao, Deo Shinyanga aliyesema makada hao wametoka katika majimbo 25 ya mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza na wamechanga Sh100,000 kwa ajili ya fomu hiyo.
Uaminifu wa Wenje ndani ya chama hicho, ndiyo sababu iliyotajwa na kundi la wanachama hao kumchukulia fomu.
Katika uchaguzi huo Wenje atachuana na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) John Pambalu ambaye ameshachukua fomu kuwania kiti hicho akisisitiza kanda ya Victoria inahitaji mabadiliko.
Msigwa
Wakati la Wenje halijapoa wafuasi wa Msigwa walifuata. Hawa walikuwa wanawake kutoka mikoa ya Mbeya, Rukwa, Songwe na Njombe na walimpelekea nyumbani kwake Iringa.
"Tunaimani kubwa na Mchungaji Msigwa amefanya kazi kubwa ndani ya kanda ya Nyasa, tunamhitaji yeye kuliko anavyotuhitaji sisi," alisema mmoja wa wanawake hao, Christina Kananda.
Kutokana na hilo, Msigwa alisema: "Ni heshima kwangu kwa watu wanaoniunga mkono kuchanga fedha na kunichukulia fomu naheshimu uamuzi wao. Nina thamani mchango wao wamenipa nguvu zaidi ya kuongeza kasi ta kutekeleza majukumu yangu nitakapoibuka kidedea."
Sugu
Sugu naye hakupoa baada ya vijana wa Bavicha wa mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe, Songwe na Rukwa kujitokeza kumchukulia fomu, kama ilivyokuwa kwa akina Wenje na Msigwa.
Katibu wa Bavicha mkoa wa Mbeya, Ahobokile Mwangosi alisema ni vijana 30 ndiyo waliokwenda kuchukua fomu hiyo kumuunga mkono Sugu.
“Sasa tupo katika maandalizi ya mwisho ya kwenda ofisi za kanda kumchukulia fomu Sugu, yote ni harakati za kujenga chama tunaamini mgombea tunayemuunga mkono ndiye mtu sahihi kwa sasa kuwania nafasi hii,” alisema.
Kwa mtazamo wa Mwangosi, hatua iliyofika kanda hiyo Sugu anastahili kuiendeleza.
Mwangosi alisema Sugu amekuwa msingi mzuri wa kukijenga chama hicho, kwani amekuwa akitembelea majimbo na mikoa ya kanda hiyo.
"Amefanya vitu vingi vinavyotuonyesha kwamba ni mtu sahihi, ndio maana tunaungana naye kwenye harakati hizi za kuwania uenyekiti, Sugu amehamasisha mchakato wa usajili wa Chadema kidijitali na kufanya Mbeya kuongoza," amesema Mwangosi.
Sugu ambaye ni mjumbe wa zamani kamati kuu wa Chadema atachuana na Mchungaji Msigwa kuwania uenyekiti wa kanda ya Nyasa yenye mikoa ya Njombe, Mbeya, Iringa, Songwe na Rukwa.
Sugu afunguka
Akizungumzia Mwananchi Digital Sugu amesema ,"wamenifanyia 'suprise' vijana wa Bavicha mkoa wa Mbeya na mikoa ya jirani, mimi nilikuwa na mipango kumbe na wao walipanga yao, hii inaonyesha ni sapoti ya chama katika kanda hii hata wengine sio wapiga kura.
"Hali hii inaonyesha siko peke yangu katika safari hii kuna wanachama wapo nyuma yangu hatua inayonipa nguvu zaidi, ndio maana unaona sipapaliki, nina utulivu wa hali ya katika jukumu langu linalokuja mbele," amesema Sugu.
Sugu anahitaji kuhamasisha mambo lakini wanachama wa Chadema kanda ya Nyasa wanajua uwezo wake wa uongozi na wanachokihitaji safari hii katika kanda hiyo hivi sasa.
"Kesho (Jumamosi Aprili 20) nitarudisha mwenyewe na nitazungumza kidogo ila nikishateuliwa na kamati kuu nitaeleza mengi zaidi mimi ni mtu tofauti ninayependa viwango kwa kitu ninachokifanya," amesema Sugu. |
Katika kutekeleza mpango wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, wauguzi kutoka Mikoa 10 nchini, wan | Katika kutekeleza mpango wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, wauguzi kutoka Mikoa 10 nchini, wanatarajiwa kupatiwa majiko ya gesi.
Hatua hiyo inakuja katika kipindi ambacho Serikali imeweka mpango wa kuhama kutoka matumizi ya nishati chafu kwenda safi kwa ajili ya kupikia.
Tangu kuanza kwa mpango huo, wananchi wa maeneo mbalimbali wameshuhudiwa wakikabidhiwa majiko ya gesi kwa ajili ya kuendana na mabadiliko hayo.
Hayo yameelezwa leo Ijumaa, Aprili 19, 2024 na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel katika hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya utoaji wa majiko hayo kati ya taasisi hiyo na Kampuni ya gesi ya Oryx iliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala.
Amesema lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha wanawaepusha wahudumu hao na athari za matumizi ya nishati zisizofaa, ili waendelee kutoa huduma kwa wananchi.
Kwa mujibu wa Doris, ugawaji wa majiko hayo utafanyika kwa wauguzi kutoka Mikoa 10 nchini.
“Tunatambua nafasi ya wauguzi wa afya, wamekuwa na mchango mkubwa kwenye jamii, tunaona makundi mengine yakipewa majiko sisi tunaona ni muhimu tuwape wauguzi,” amesema.
Ameeleza majiko hayo yatakabidhiwa kwa wauguzi waliopo katika mazingira magumu, ili waepuke matumizi ya nishati zisizofaa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mwananyamala, Zavery Benela amesema matumizi ya nishati chafu ni moja ya sababu ya magonjwa mengi ya mfumo wa hewa kwa binadamu.
Ameeleza kati ya wagonjwa 500 wa nje wanaopokelewa katika hospitali hiyo, zaidi ya nusu wanasumbuliwa na magonjwa ya mfumo wa hewa.
“Haya ndiyo magonjwa namba moja kwa wagonjwa wengi kwenye hospitali yetu, tumekuwa tukiwapokea na ukiuliza namna anavyoishi utakuta anatumia nishati isiyofaa kupikia,” ameeleza.
Mkurugenzi Mkuu wa Oryx, Benoit Araman amesema matarajio yao ni kuhakikisha kila Mtanzania anatumia nishati safi kwa ajili ya kupikia.
“Kunahitajika elimu ya kuhakikisha watu wanaokolewa dhidi ya matumizi ya nishati isiyofaa, tunatarajia kutoa majiko mengi zaidi na hadi sasa tumeshatoa majiko 32,000,” amesema. |
Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba amesema msingi wa kuimarisha muungano katika miaka 60 ijayo ni k | Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba amesema msingi wa kuimarisha muungano katika miaka 60 ijayo ni kuhakikisha sera na mipango inayowekwa kwa pande zote mbili inajali maslahi ya wananchi, badala ya madaraka.
Katika kauli yake hiyo, amesema msisitizo wa mijadala kuhusu muungano isijikite kwenye siasa, bali kwa sasa ni vema kuona namna bora ya kuwahudumia wananchi, ili wote wajione Watanzania na si kujitofautisha.
Warioba anakuja na kauli hiyo katika kipindi ambacho Tanzania inakaribia kuadhimisha miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mataifa hayo yaliungana Aprili 26, mwaka 1964, Tanganyika ikiwa chini ya Rais wake wa kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, huku Zanzibar ikiwa chini ya Abeid Amani Karume ambao ndio waasisi wa Muungano huo.
Jaji Warioba alitoa kauli hiyo nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa habari katika mahojiano maalum kuhusu miaka 60 ya Muungano yaliyoandaliwa na Idara ya Habari Maelezo.
Uwaguse wananchi
Kwa mtazamo wa Jaji Warioba, kipindi kijacho Serikali inapaswa kujikita katika kuimarisha haki za Watanzania ndani ya muungano.
Katika utekelezaji wa hilo, kiongozi huyo aliyewahi kuwa Makamu wa kwanza wa Rais, alieleza ni vema kuangalia mambo ya maendeleo yenye utofauti ili hatua zichukuliwe.
Alitolea mfano upatikanaji wa huduma za afya, ingawa si jambo la muungano lakini mwananchi kutoka upande wowote anapaswa kuwa na uhuru wa kupata huduma hiyo popote.
“Inatakiwa mwananchi wa bara akiwa na bima ya afya itumike hata atakapokwenda hospitali ya Zanzibar na bima ya Zanzibar itumike hata bara,” alisema.
Msingi wa muungano kwa mujibu wa Jaji Warioba ni kuwaunganisha watu wa pande zote ili kila mmoja ajione yupo nyumbani anapokuwa popote na awe huru kufanya shughuli yoyote.
“Kama ni kilimo anaweza akaenda popote kufanya shughuli yoyote na hiyo ndiyo faida ya muungano wananchi wapate umoja,” alisisitiza.
Ukiachana na sekta ya afya, mkongwe huyo wa siasa alitaja uchumi wa buluu na utalii kuwa baadhi ya sekta nyingine zinazopaswa kuwekewa sera moja na utekelezwaji wa mipango yake uwe shirikishi kwa Serikali zote.
“Kama kuna mtu ametaka nje anataka anataka kwenda mbugani aanzie huko kisha ataenda kwenye fukwe Zanzibar, ndiyo vizuri kwanza tutahamaisha utalii na kutengeneza ajira zaidi," alisema.
Alisisitiza mambo yote yanayowahusu wananchi lazima yaunganishwe kuwa kitu kimoja, ili kuimarisha muungano.
Alisema hata rasimu ya mabadiliko ya Katiba inayoeleza kuhusu uwepo wa Serikali tatu, imebainisha uwepo wa tume itakayounganisha nchi na kushauri kuhusu mambo ya kisera.
“Usipokuwa na sera moja mambo yatakuwa tofauti, mambo yote yanayohusu shughuli za wananchi lazima yaunganiashwe kuwa moja,” alisema.
Kero za muungano
Jaji Warioba alionyesha mtazamo tofauti kuhusu kero za muungano, akisema nyingi zinazozungumzwa ni masuala ya kisiasa na madaraka, haziwahusu wananchi wa kawaida.
Alikwenda mbali zaidi na kueleza hata Serikali inapotangaza kufuta baadhi ya kero, mara nyingi wananchi hawafahamu ni zipi na hawapaswi kuhusishwa nazo.
“Ukiuliza wananchi wanazijua hizo kero, ni Serikali pekee ndiyo inayozungunza na haielezi ni zipi. Nataka watu watoke kwenye kuzungumzia madaraka wakati wote, tayari uhusiano wa wananchi umeimarishwa ni vema kuimarisha zaidi ili wajione kuwa wote ni Watanzania,” alisema Jaji Warioba.
Lugha za viongozi
Katika mahojiano hayo, Warioba aligusia kile alichokiita kauli za baadhi ya viongozi, akisema nyingi zinaugawa muungano badala ya kutengeneza umoja.
“Kinachopaswa kuangaliwa ni maslahi ya nchi na hata viongozi kwa sasa wamekuwa na lugha za kuzungumzia pande mbili ilhali wanapaswa kuzungumza kuhusu Tanzania kwa ujumla.
"Wanataka kama tusiendelee mimi nasema tukitatua changamoto za wananchi wa kawaida wao hawataangalia upande gani," alisema.
Alitaka yaangaliwe mambo yanayoimarisha muungano sio yale yanayofanya nchi zitengane kabisa.
Mwelekeo kuhusu uchaguzi Zanzibar
Katika moja ya majibu yake ya maswali ya waandishi wa habari, Jaji Warioba alisema umefika wakati Zanzibar inapaswa kufanya mabadiliko ya kisiasa kwa maslahi ya muungano.
“Umefika wakati Zanzibar sasa ingeanza kufanya mabadiliko ya kisiasa, kwa sababu ya mazingira ya mapinduzi ililazimika kuweka mambo fulani fulani ilikuwa ni muhimu kwa wakati huo,” alisema.
Miongoni mwa mambo aliyosema yanapaswa kubadilishwa ni sheria inayomtambua mzanzibari aliyeishi kwenye eneo husika kwa miaka mitatu ndiye anayepaswa kupiga kura katika eneo hilo.
Alisema hilo linawabagua Wazanzibari wanaoishi nje ya visiwa hivyo, akisisitiza ni vema kufanyia mabadiliko.
“Kwa sasa kuwe na masharti nafuu kwa dayaspora wawe na haki ya kupiga kura na kuna nchi kukiwa na uchaguzi unawaona raia wao wanaoishi Tanzania wanapiga kura, nasi tuwe na hiyo,” alisema.
“Zanzibar waanze kufikiria kuona kama utaratibu huo wanapaswa kuendelea nao au wasiendelee, hayo ndiyo mambo yanayohusu wananchi na yanapaswa kutatuliwa,” alisema.
Alisisitiza kila kinachofanyika, mwelekeo wake uwe kwenye kuwaunganisha wananchi ili hata ikifika miaka 100 wote wajione ni Watanzania.
Uzoefu wa mataifa mengine
Baada ya uchaguzi wa mwaka 1980, alisema Mwalimu Nyerere alimtu yeye na Pius Msekwa kwenda kujifunza kuhusu muungano katika mataifa yenye uzoefu.
Katika safari hiyo, alisema walikwenda Uingereza ambako pamoja na kukuta kila eneo lina utamaduni wake, wananchi wote walitambulika kwa taifa moja.
Hali kama hiyo, alisema aliikuta Marekani na hata Canada na India walikokwenda kutekeleza maelekezo hayo ya Mwalimu Nyerere.
"Serikali yoyote ile lazima ihudumie wananchi, kwa wananchi tazameni haki zao sio kutazama mambo ya muungano, hata lisipokuwa jambo la muungano lazima muagalie,” alisema Jaji Warioba.
Changamoto zilizokuwepo
Alisema baada ya Tanganyika na Zanzibar kuungana, changamoto iliyokuwepo ni katika kukusanya mapato na kuyagawa kwa ajili ya Serikali ya muungano na kuyaacha mengine kwa ajili ya Zanzibar.
Changamoto hiyo, alisema ilisababisha kufanywe mabadiliko yaliyoiruhusu Zanzibar kukusanya kodi hizo kisha yenyewe iwasilishe mchango wa muungano.
Pamoja na mabadiliko hayo, alieleza bado kulikuwa na changamoto kwa sababu Zanzibar haikuwa inawasilisha fedha hizo.
“Matatizo yalibaki hapo kwa kuwa Zanzibar haikuwa inaleta mchango na sina uhakika kama hilo limerekebishwa,” alisema.
Hata hivyo, alieleza kujivunia kwake muungano kwa kuwa umeunganisha wananchi na ndiyo iliyokuwa sababu ya kuungana.
Alisema ili kuupima muungano ni vema kuangalia faida kwa wananchi na ikitokea wananchi hawajalalamika ujue hakuna tatizo.
Alisema ushahidi wa uimara wa muungano ni uwepo wa muingiliano wa wananchi, akifafanua kuna Wazanzibari wengi wanaoishi bara.
Katika maelezo yake, Jaji Warioba alisema kitu pekee kinachozungumzwa na wananchi katika muungano ni muundo wake, akisisitiza kuna umuhimu wa kuamua.
"Watanzania wote wanapenda muungano, nikipata bahati ya kuzunguka nchi hii wakati wa kutafuta maoni ya wananchi moja ya mambo yaliyozungumzwa ilikuwa ni muungano," alisema. |
Uimara katika usimamizi wa sekta fulani na kuwa na mchango katika taifa lake ni miongoni mwa sababu | Uimara katika usimamizi wa sekta fulani na kuwa na mchango katika taifa lake ni miongoni mwa sababu zilizotajwa na wasomi kuwa chachu ya Rais Samia Suluhu Hassan kutunukiwa shahada ya nne ya heshima ya udaktari.
Kwa mujibu wa wasomi hao, mara nyingi shahada hizo hutolewa kwa mtu aliyeonyesha mchango mkubwa katika taifa lake na hata kuivusha nchi katika mambo magumu.
Pamoja na hayo, wanazuoni hao wameeleza wakati mwingine hutolewa kama mbinu ya taifa husika kufanikisha mambo yake.
Mitazamo hiyo ya wasomi inakuja wakati ambao, Rais Samia ametunukiwa shahada nne za heshima za udaktari tangu alipoingia madarakani Machi mwaka 2021.
Shahada ya kwanza ya heshima ya udaktari, alitunukiwa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm) Novemba 30, mwaka 2022.
Hiyo ilifuatiwa na shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa kutoka Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru nchini India, Oktoba 10, mwaka jana.
Tunu ya shahada hizo haikuishia hapo, mkuu huyo wa nchi alitunukiwa shahada nyinyine ya heshima ya udaktari ya Usimamizi wa Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA), Desemba 28, 2023.
Kama hiyo haitoshi jana Rais Samia alitunukiwa shahada nyingine ya heshima na Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki.
Wasomi
Akizungumzia shahada hizo, mchambuzi wa masuala ya siasa, Buberwa Kaiza kwa kawaida shahada hizo hazina ukomo wa nani apewe na nani asipewe, bali utashi wa chuo ndiyo unaoamua.
Lakini, duniani alisema wanaopewa ni wale waliofanya mambo makubwa kwenye nchi zao, mathalan viongozi waliozipitisha nchi zao kwenye mambo magumu.
“Shahada hizi zinaweza kutolewa kutoka kwa watu wenye maslahi na Tanzania, inakua kama njia ya kusukuma mambo yao,” alisema.
Hata hivyo, Kaiza alisema haoni kama shahada hiyo inaongeza lolote kwa Watanzania.
Mbali na Buberwa mwingine aliyezungumzia shahada hizo ni mchambuzi wa Sayansi ya Siasa, Dk Paul Loisulie aliyesema shahada ya heshima hupewa mtu pale anapotoa mchango mkubwa kwa nchi yake katika sekta fulani.
“Ni heshima ambayo chuo chenyenye huamua kumpa muhusika, na ni utaratibu uliopo duniani kote. Ni kama wameamua kumpa maua yake kwa kile anachokifanya kwenye eneo fulani,” alisema.
Hata hivyo, mwanazuoni huyo alisema kwa maana nyingine shahada kama hizo hutumika kama mbinu za nchi fulani kushawishi kufanikishwa kwa mambo yao.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Justine Kajerero alisema shahada hizo hubadili hadhi ya mtunukiwa kama ambavyo Rais Samia anatambulika kama Daktari kwa sasa.
“Kwa taifa tumeona utendaji wake, na ni vizuri kwamba anatambuliwa ulimwenguni,” alisema.
Kajerero alisema mara nyingi kutolewa kwa shahada hizo kunahusisha majopo na kamati za vyuo husika yanayokaa kujadili kwa kina kama muhusika anastahili kabla ya kumtunuku.
“Hii inaweza kumfanya afanye mambo makubwa zaidi kwenye hiyo sekta ambayo imetambuliwa na kumfanya apate heshima hiyo,” alisema.
Rais Samia
Akizungumza baada ya kutunukiwa shahada hiyo, Rais Samia alisema ni heshima kwake na taifa lake kutambuliwa na chuo hicho hadi kutunukiwa shahada hiyo.
“Hii ni heshima kwangu na furaha kwa nchi yangu. Ninachofurahi zaidi ni kuona mambo ninayoyafanya nchini kwangu yanaonekana na ulimwengu mzima,” alisema.
Katika hotuba hiyo, Rais Samia alisisitiza Tanzania na Uturuki kuimarisha uhusiano kwa maslahi ya kiuchumi kupitia uwekezaji.
Hata hivyo, alieleza kuwepo kwa mwenendo mzuri wa uhusiano wa mataifa hayo, kwani hata urari wa biashara umeongezeka kutoka Dola za Marekani 60 milioni mwaka 2012 hadi Dola za Marekani 300 milioni mwaka 2022/23.
Alitumia juukwaa hilo, kueleza juu ya kuimarika kwa uchumi wa Tanzania na juhudi za Serikali katika kuweka mazingira bora na rafiki kwa wawekezaji.
Alisema leo wanatarajia kufanya mkutano wa kibiashara na jumuiya za wafanyabiashara jijini Istanbul nchini humo.
Hata hivyo, alieleza aliingia madarakani katika kipindi ambachod dunia ilikuwa inakabiliwa na janga la Uviko-19 na vita vya Urusi na Ukraine, lakini hatua mbalimbali zilichukuliwa kuhakikisha ustawi unaendelea.
“Nina furaha kueleza mwaka 2023 mfumuko wa bei ulibaki kawaida kwa maana asilimia 3.9 na pato la taifa lilifikia asilimia 5.2,” alisema. |
Shughuli ya kuendesha bodaboda kwa mkataba imeingiwa na majanga, baada ya malalamiko ya madereva dhi | Shughuli ya kuendesha bodaboda kwa mkataba imeingiwa na majanga, baada ya malalamiko ya madereva dhidi ya wamiliki wakidai kupewa mikataba ya kinyonyaji.
Hatua hiyo kwa mujibu wa madereva hao, inasababisha wengi waishie kunyang’anywa bodaboda wanapokaribia kumaliza mikataba hiyo na hivyo, wanabaki kuwa watumwa wa wamiliki katika maisha yao yote.
Pamoja na malalamiko hayo, wamiliki nao wanarudisha lawama kwa madereva, wakiwatuhumu kukosa ustaarabu katika utunzaji wa vyombo hivyo vya moto na uaminifu katika uwasilishaji wa mapato.
Katika mikataba hiyo inayosainiwa katika Serikali za Mitaa/ Vijiji, mmiliki humkabidhi dereva pikipiki kwa ajili ya kupakia abiria kwa sharti la kuwasilisha mapato ya kila wiki kwa muda wa mwaka mmoja au miezi 16, kisha bodaboda hiyo inakuwa mali yake.
Hata hivyo, hali hiyo ya kutupiana lawama kati ya pande hizo mbili, imeibua hoja ya kukosekana kwa ajira nchini, iliyotajwa kuwa sababu ya vijana wengi kuishia kwenye shughuli hiyo ya bodaboda, pamoja na changamoto zilizopo.
Malalamiko ya bodaboda kuhusu changamoto hizo, yaliibuliwa mkoani Mara juzi katika ziara ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana.
Malalamiko madereva
Akitoa malalamiko yake kuhusu hilo mmoja wa madereva wa bodaboda mkoani humo, Joseph Chege alisema pamoja na kwenda katika halmashauri kulalamika hawakupatiwa ufumbuzi.
Kinachochagiza malalamiko yao, alieleza ni kiasi cha fedha wanachotakiwa kuwasilisha kwa mmiliki kwa wiki ambacho ni Sh70,000 ndani ya miezi 16.
Alisema wanatakiwa kuwasilisha kiasi hicho cha fedha ilhali, bei halisi ya pikipiki dukani ni Sh2 milioni, hivyo kwa miezi 16 wanamuingizia mmiliki Sh4.8 milioni.
“Ukifanya kazi kwa muda huo chombo kinakuwa kimechoka hata ukifika wakati wa wewe kukimiliki hakikupi faida tena,” alisema Chege.
Dereva mwingine aliyelalamikia hilo ni Shadrack Mwita aliyesema matajiri wengi hununua pikipiki kwa shughuli hiyo, hasa wanapoona vijana wanahitimu vyuo na kurudi mitaani.
“Hapa Bunda ukitaka kuendesha pikipiki, mkataba wake kwa wiki Sh70,000 unatakiwa kuitoa ndani ya miezi 16, pamoja na ugumu huo unaweza ukakuta umepambana umebakiza miezi miwili umepata changamoto anafuta mkataba na kukunyang’anya chombo chake,” alisema.
Suala la kusitishiwa mikataba inapokaribia mwishoni, liliibuliwa na Wambura Marwa na bodaboda wengine waliokuwepo katika mkutano huo.
Malalamiko hayo yanapigiwa msumari na Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa wa Dar es Salaam, Michael Massawe aliyesema mikataba wanayopewa imeegemea upande wa wamiliki na kumnyima haki dereva.
Katika mikataba hiyo, Massawe alisema kuna vipengele vinavyoomuadhibu dereva ikiwemo kunyang’anywa pikipiki iwapo atakosea, lakini hakuna kinachomuadhibu mmiliki atakapotenda makosa.
“Maana yake dereva tu kwa sababu hana kitu ndiye anayeonekana atakosea, lakini mikataba hautambui kuwa kuna wakati mmiliki anaweza kukosea,” alisema.
Mazingira hayo, alisema ndiyo yanayorahisisha wamiliki kuwanyang’anya pikipiki madereva hasa pale wanapokaribia kumaliza mikataba.
Suala la kukosekana ustaarabu limeibuka hata kwa wamiliki, akisema baadhi wanapokosa sababu ya kumnyang’anya pikipiki dereva huamua kumtumia watu wampige na kumnyang’anya.
Hata hivyo, Massawe alipendekeza utaratibu huo unapaswa kufanywa kupitia benki ili kurahisisha ukopeshaji na malipo.
Alisema tayari Mkoa wa Dar es Salaam umefanikiwa katika hilo na madereva takriban 3,000 wamekopeshwa pikipiki kwa mfumo huo.
“Tunachotamani ni Serikali iingilie kati na kuamua kuwakopesha vijana pikipiki hizi kupitia benki hii itasaidia kwa sababu kule hakutakuwa na mikataba ya kinyonyaji,” alisema.
Wamiliki walia ustaarabu
Wakati vijana hao wakilalamikia hayo, wamiliki wa bodaboda nao wanarudisha lawama kwa madereva, wakisema wengi wao si wastaarabu kama inavyofafanuliwa na Abdul Msonga mmoja wa wamiliki wa bodaboda aliyewahi kufanya biashara hiyo.
Msingi wa kauli ya Msonga ni kile alichoeleza, madereva wengi wa bodaboda hawana leseni na wanapokamatwa hukimbia na kuiacha pikipiki kwa askari wa usalama barabarani.
“Iliwahi kunitokea amekamatwa na askari, amekimbia akaacha pikipiki ilibidi niifuate na kugharimia faini ya makosa yake, nikamnyang’anya,” alisema.
Kukosa leseni ni jambo moja, lakini kulimbikiza deni la malipo ya wiki kwa mujibu wa masharti ya mkataba wanayoandikishiana ni tatizo lingine lililopo kwa madereva hao wa bodaboda, kwa mujibu wa Msonga.
Alisema idadi kubwa ya madereva hao hawawasilishi mapato kwa mujibu wa makubaliano ya mikataba, badala yake wanajiamria kutoa kwa matakwa yao.
“Mimi na dereva wangu masharti ya mikataba wetu yalikuwa, akishindwa kuwasilisha mapato kwa wiki mbili nachukua pikipiki yangu.
“Pamoja na masharti hayo, lakini dereva wangu alikuwa anapitisha hadi mwezi bila kuniletea kiasi chochote cha fedha, ulifika wakati, muda wa mikataba umeisha lakini bado namdai fedha za miezi minne, ilibidi nimnyang’anye,” alisema.
Mmiliki mwingine wa bodaboda anayetoa kwa mkataba, Benson Msaky alisisitiza kilichoelezwa na Msonga akisimulia mikasa aliyokutana nayo baada ya kuwapa pikipiki madereva hao.
Msaky alisema baada ya kukabidhi pikipiki kutoka dukani, mambo yalianza kwa dereva huyo kuuza baadhi ya vifaa likiwemo betri na skockup na alinunua vilivyotumika na kuvifunga.
“Ameuza betri la pikipiki iliyotoka dukani na shockup akanunua vilivyotumika akavifunga, pikipiki ilianza kusumbua kila siku. Nilipofuatilia nikabaini ameuza vifaa halisi amenunua vingine,” alisema.
Mbali na hilo, alisema dereva mwingine alikuwa anawapa watu pilipiki wapakie abiria kisha wampelekee fedha ndipo aziwasilishe kwa mmiliki ‘Day Worker.’
“Sio tatizo kwa kuwa mimi nachotaka ni fedha, lakini shida inakuja kwenye utunzaji, hawa wanaowapa hawatunzi chombo na wanabeba mizigo hata inayozidi uwezo wa pikipiki, ndani ya miezi miwili pikipiki inachoka mno,” alisema.
Lakini utunzaji wa chombo nao ni jambo lingine lililotajwa na wamiliki kuwa changamoto iliyopo kwa madereva hao na hivyo kusababisha wanyang’anywe pikipiki.
Hata hivyo, kauli hiyo ya wamiliki imejibiwa na Massawe akisema wanajitetea lakini uhalisia ni kwamba wanawanyonya madereva.
Alisema madereva wengi huwa wanahakikisha usalama wa vyombo hivyo kwa kuwa wanafahamu ndiyo maisha yao ya baadaye.
“Unakuta bodaboda au bajaj inakaribia kumaliza mikataba inaonekana vizuri kama imetoka jana dukani,” alisema.
Kuhusu uaminifu kwenye kufanya marejesho, alisema inatokea kwa dharura ikiwemo dereva anapoumwa au kupatwa na tatizo lolote.
“Mkataba hauelezi chochote kuhusu dereva atakapoumwa, mmiliki anataka apelekewe fedha hata kama unaumwa, ndiyo maana tunasema mikataba mibaya,” alisema.
Tatizo ni ajira
Unaweza kujiuliza kwanini vijana wanang’ang’ana na shughuli hiyo pamoja na changamoto zilizopo, lakini uhaba wa ajira na ufinyu wa fursa za kujipatia kipato ndiyo jawabu lake, kama inavyoelezwa na Mwenyekiti huyo.
Kwa mujibu wa Massawe vijana wengi wenye umri wa kuanzia miaka 18 hadi 35 walioshindwa kuendelea na elimu ya sekondari, elimu ya juu na hata waliohitimu na kukosa ajira, wamekimbilia kwenye bodaboda.
“Kwa mazingira ya Tanzania ajira hakuna kuna idadi kubwa ya vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 35 wanashindwa kuendelea na elimu wanarudi mtaani na hata wanaomaliza vyuo wanarudi huku kwa kukosa ajira.
“Wanaona bora waje kwenye bodaboda angalau kuponea machungu yao. Kwa hiyo hatuna namna ya kufanya ndiyo maana tuning’ang’ana licha ya changamoto zilizopo,” alisema.
Kinachozungumzwa na Massawe kinashabihiana na mwanazuoni wa uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Profesa Abel Kinyondo aliyesema kumekosekana mbadala wa kazi ndiyo maana vijana wanaishia kufanya shughuli hiyo.
Kwa mtazamo wa mwanazuoni huyo, shughuli ya udereva bodaboda ni moja ya ajira zisizo na staha kwa vijana.
"Haipaswi kuwa ajira kwa kuwa haina malengo, kuna watu wanatetea bodaboda imekuwa ajira yao na wengi wanaofanya kazi hiyo si kwamba wanapenda ni vile hawana mbadala kwa sababu hakuna ajira," alisema.
Alisisitiza hatua ya vijana kuendelea na shughuli hiyo pamoja na changamoto zilizopo ni dalili ya kukosekana mbadala wa kazi.
Serikali iingilie kati
Mhadhiri mwingine wa Uchumi wa UDSM, Profesa Samweli Wangwe alisema ni muhimu Serikali ikaingilia kati kutengeneza usawa katika mikataba hiyo ili pande zote zinufaike.
Hata hivyo, msomi huyo alitilia shaka suala la bodaboda ya Sh2 milioni kuingiza faida ya Sh5 milioni, akisema ni kubwa isiyolingana na uzalishaji halisi wa chombo husika.
“Haiwezekani ununue chambo Kwa Sh2 million alafu umpatie mtu aendeshe na utengeneze faida mara mbili zaidi ni faida kubwa mnoo ilitakiwa Serikali isaidie kuingia makubaliano ili wapate hata faida ya Sh1.6 milioni ili na wanaofanya kazi nao wafaidike," alisema.
Alichosema Kinana
Akizungumza katika ziara yake hiyo kuhusu malalamiko ya bodaboda hao, Kinana aliahidi kuzungumza na wabunge ili watengeneze utaratibu mzuri kuhusu hilo.
“Vijana wanahoja, nimekubaliana nanyi, nitaenda kuongea na Wabunge wote kuhusiana na suala hili ili kutengeneza utaratibu mzuri wa kuwakopesha vijana pikipiki na kukabiliana na watu wanaowanyonya vijana,” alisema.
Hata hivyo, alisema wanaofanya hivyo ni wale wachache wanaotaka kujinufaisha huku wakiwanyonya wengine, akisisitiza haiwezekani pikipiki ya Sh2 milioni ikaingize Sh5 milioni.
"Jambo hili si sawa, mjini hapa shughuli hii inafanywa na Wachina, nitaenda kuongea nao, shida ilivyo sasa wanakopesha mtu mmoja halafu yeye anakuja kuwanyonya vijana apate Sh5 milioni kila moja, huku ni kuwafirisi vijana," alisema. |
Mtindo wa wapigakura kuwachukulia fomu wagombea ndilo jambo linaloonekana kuchagiza uchaguzi wa wana | Mtindo wa wapigakura kuwachukulia fomu wagombea ndilo jambo linaloonekana kuchagiza uchaguzi wa wanaowania nafasi mbalimbali katika Kanda nne za Chadema.
Katika mchakato wa kuelekea uchaguzi huo, imeshuhudiwa wafuasi mbalimbali wakiwalipia ada za fomu na kuwachukulia wagombea mbalimbali wanaowaunga mkono.
Hilo lilishuhudiwa Aprili 16, mwaka huu kwa nyakati tofauti ambapo wafuasi wa wagombea wawili kati ya wengi wa nafasi hizo, wakienda yalikokuwa makao makuu ya kanda husika kwa ajili ya kuwachukulia fomu.
Wagombea waliochukuliwa fomu ni Ezekiah Wenje anayetetea kiti cha uenyekiti wa Kanda ya Viktoria na Peter Msigwa anayewania kutetea nafasi yake ya uenyekiti wa Kanda ya Nyasa.
Hata hivyo, mtazamo wa wanazuoni wa sayansi ya siasa kuhusu jambo hilo, halina taswira mbaya lakini litageuka kuwa baya iwapo wanaofanya hivyo wana sababu za kidini au kikabila.
Wanaomuunga mkono Wenje
Jana makada zaidi ya 50 wanaomuunga mkono Wenje wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Geita, Deo Shinyanga walimchukulia fomu mwenyekiti huyo wa kanda anayemaliza muda wake.
Katika maelekezo yake, Shinyanga alisema waliokwenda kuchukua fomu hiyo ni wanachama kutoka majimbo 25 ya Mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza.
Mbali na kumsindikiza, wanachama hao Shinyanga alisema walichanga fedha kwa ajili ya kumnunulia fomu mgombea huyo.
"Msingi wa kuyafanya yote hayo ni kile walichoeleza, mwanasiasa huyo amekuwa mwaminifu ndani ya chama hicho tangu alipotoka bungeni mwaka 2015 bila kurudi nyuma.
“Tunao watu tuliwaamini kwa viwango vikubwa lakini mwisho wa siku wametufedhehesha, lakini Wenje amesimama. Tulikuwa na Wenyeviti wa Kanda na wamesaliti chama kwa vipande vya fedha,” alisema Shinyanga.
Kwa mujibu wa Shinyanga, Wenje alisimama na chama hicho katika nyakati zote za furaha na zile ngumu hivyo, wanamuona anastahili wadhifa huo.
“Tumeamua kumfariji kwa kumuunga mkono kwa aliyoyafanya kwa Chadema,” amesema.
Pamoja na Wenje, wanaowania nafasi hiyo katika kanda hiyo ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), John Pambalu.
Hata hivyo, Mwananchi imearifiwa tayari Pambalu alishachukua fomu katika ofisi za chama hicho mkoani Kagera, akiambatana na wafuasi wake 100, lakini yeye alikwenda kuchukua mwenyewe.
"Nimeamua kuchukua mwenyewe bila kutuma watu, kinachofuata ni kuijaza na kuirejesha kisha nasubiri uteuzi katika ngazi husika," alisema Pambalu.
Msigwa na washindani wake
Msigwa naye anacho kibarua cha kuchuana na Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ katika Kanda hiyo ya Nyasa.
Akizungumza baada ya kuchukuliwa fomu, Msigwa alisema: "Ni heshima kwangu kwa watu wanaoniunga mkono kuchanga fedha na kunichukulia fomu naheshimu uamuzi wao. Nina thamani mchango wao wamenipa nguvu zaidi ya kuongeza kasi ta kutekeleza majukumu yangu nitakapoibuka kidedea," amesema Msigwa na Mwananchi.
Mbali na hao, mgombea mwingine wa nafasi hiyo ni Emmanuel Ntobi aliyesema atakwenda kuchukua fomu mwenyewe na wakati wa kuirudisha ndipo ataambatana na wapambe.
"Kesho nitakwenda kuchukua fomu, nimedhamiria kuleta mageuzi katika kanda ya Serengeti," alisema Ntobi ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema mkoani Shinyanga.
Mtazamo wa kisomi
Mwanazuoni wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Conrad Masabo alisema hilo si jambo baya iwapo msingi wake ni mapenzi ya wafuasi kwa mgombea husika.
Lakini, alisema itakuwa mbaya iwapo wanaoamua kumchukulia fomu mgombea huyo wanashinikizwa na sababu za kikabila au udini.
“Kama msingi wa wafuasi wanaomchukulia fomu mgombea ni kwa sababu wanapenda misimamo na uongozi wake, ni dhahiri baada ya uchaguzi hakutakuwa na mpasuko.
“Lakini itakuwa mbaya iwapo watu wanamchukulia mtu kwa vigezo vya kidini na kikabila, kwa maana nchi yetu inaweza kutengeneza tatizo kubwa kwenye siasa,” alisema.
Kadhalika, mwanazuoni huyo alisema kwa mtazamo wa siasa za Tanzania, jambo hilo linachagiza uchaguzi na kuonyesha nani anapendwa zaidi. |
Unapotaja orodha ya vyama vya siasa vyenye umri mdogo nchini, ACT Wazalendo ni miongoni mwavyo, inga | Unapotaja orodha ya vyama vya siasa vyenye umri mdogo nchini, ACT Wazalendo ni miongoni mwavyo, ingawa muda kiliyoishi unahusisha mambo mengi yanayokipa taswira isiyolingana na uchanga wake.
Licha ya umri wake mdogo, ACT Wazalendo ni moja kati ya vyama vitatu vikubwa nchini na hilo linathibitishwa na wingi wa wafuasi wake, kadhalika uwakilishi kilionao katika vyombo vya maamuzi.
Chama hicho kilipata usajili wa kudumu mwaka 2014, kwa hesabu za haraka haraka mwaka huu kinatimiza miaka 10, umri ambao ukiufananisha na binadamu, tayari ameanza kujitambua na anakaribia rika balehe.
Kwa mtazamo wangu ndicho chama chenye umri mdogo kilichofanikiwa kujenga ushawishi na kuwa mwalimu wa siasa za kitaalamu kwa vyama vingine, kadhalika kimeonyesha namna na umuhimu wa kuwatumia wataalamu katika siasa.
Hayo yanathibitishwa na utaratibu wake wa kujega hoja kupitia wale kinaowaita Mawaziri Kivuli wa kila sekta, ambao mara nyingi ni wanataaluma wa sekta hizo.
Katika ujenzi wa hoja hizo, chama hicho kimekacha mtindo wa siku zote wa siasa za vyama vya upinzani nchini, unaoishia kuonyesha kasoro za utendaji serikalini, badala yake chenyewe kimejipambanua kwa kuja na suluhisho la kasoro hizo.
Achana na usahihi wa kinachopendekezwa na chama hicho, hatua pekee ya kufikiria mbinu mbadala ya kuondoa kasoro iliyopo ni tafsiri halisi ya siasa za kitaalamu na kwamba imeshuhudiwa mara kadhaa Serikali ikiyafanyia kazi mapendekezo yake.
Ni moja ya vyama vilivyopitia misukosuko ya kisiasa kama ilivyo kawaida ya safari katika siasa, kwa uchanga wake ungedhani ndiyo ingekuwa hatma ya uhai wake katika majukwaa ya kisiasa kama inavyoshuhudia kwa baadhi ya vyama, lakini bado kinasonga.
Miaka 10 iliyopita wakati kinaanzishwa, nilichukulia kawaida, sikuwa na matumaini kama kingedumu hadi sasa, nilidhani kingejifia au kufifia vya kutosha.
Hiyo inatokana na ukweli kwamba, kilianza katika nyakati ambazo siasa za Tanzania zilionekana kama za vyama viwili yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuondoa upande wa Zanzibar ambako CCM ilikuwa inashindana zaidi na Chama cha Wananchi (CUF).
Pamoja na mikakati ya kujenga ushawishi na ushindani katika siasa za Tanzania, kilichoitokea CUF mwaka 2019 cha wanachama wake wengi kuhamia ACT Wazalendo kilionyesha tafsiri halisi ya kufa kufaana.
Katika kipindi hicho, ndipo ACT Wazalendo iliposhuhudiwa kukua na kujenga ushawishi zaidi wa wafuasi, hayo yalihudiwa zaidi hasa pale mwanasiasa, Maalim Seif Sharif Hamad alipojiunga nacho.
Kujiunga kwa Seif katika chama hicho, ndiko kulikofuta ramani ya CUF katika siasa za Zanzibar na sasa ACT Wazalendo ndicho kilichobaki kuwa mshindani mkuu wa CCM katika visiwa hivyo.
Ninapoeleza kuhusu ukubwa wa chama hicho, nahusisha mambo lukuki, tukumbuke ACT Wazalendo ni sehemu ya Serikali ya Zanzibar, kina Makamu wa Kwanza wa Rais aliyetokana na Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).
Hatua hiyo imefikiwa kutokana na nafasi kiliyoipata katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 na hivyo kujumuishwa katika Serikali.
Haya yote ni machache kati ya mengi yanayokihusu chama hicho katika siasa zake za miaka 10 tangu kilipozaliwa na hiyo inatafsiri mwanzo wa miaka 10 ijayo iwapo kitaenenda kama kilivyofanya miaka 10 iliyopita.
Siasa za midahalo ni utambulisho mwingine wa chama hicho, hata katika chaguzi zake za ndani kimeshuhudia kikifanya midahalo kwa wagombea wake.
Hii inakifanya kuwa kielelezo cha siasa zinazotarajiwa na sehemu kubwa ya wanasiasa wanaohitaji ushindani, lakini hii ni fursa ya kuwajengea uzoefu wagombea katika mbinu za kujenga hoja.
Licha ya mafanikio yote, changamoto inayotazamwa kwa sasa ni maisha ya ACT Wazalendo bila muasisi wake, Zitto Kabwe kuwa ndani ya uongozi wa chama hicho.
Ingawa halionekani ombwe kubwa la uongozi, kwa kuwa mtindo wa siasa wa chama hicho umewajenga wengi kurithi nafasi hiyo na waliopo sasa si haba.
Kabwe ndiye aliyekiasisi chama hicho na ndiye aliyekuwa Kiongozi wa chama hicho, akikiongoza kwa miaka 10.
Chama hicho kwa sasa kinatarajia kufanya maadhimisho ya miaka 10 ya kuanzishwa kwake, ambayo pamoja na mambo mengine yatahusisha mijadala na shughuli mbalimbali za kijamii.
Maadhimisho ya kuzaliwa kwa chama hicho, yanaanza Aprili na kutamatika Mei 5, mwaka huu Ujiji mkoani Kigoma.
Shughuli za kijamii, mijadala na mikutano ya hadhara ni baadhi ya mambo yatakayofanyika katika wiki kadhaa za sherehe hizo. |
Kama utaifananisha safari ya miaka 60 kwa maisha ya binadamu, basi atakuwa amekaribia umri wa kustaa | Kama utaifananisha safari ya miaka 60 kwa maisha ya binadamu, basi atakuwa amekaribia umri wa kustaafu utumishi wa umma, ndivyo unavyoweza kusema kuakisi uhalisia wa umri wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Muungano wa mataifa hayo yaliyounda jina Tanzania, ulifanyika Aprili 26, mwaka 1964 chini ya waasisi wake, Mwalimu Julius Nyerere kwa upande wa Tanganyika na Sheikh Abeid Amani Karume kwa Zanzibar na sasa umefikisha umri wa miaka 60.
Maisha ya wananchi wa mataifa hayo kabla ya muungano, yalikuwa mithiri ya shubiri, ingawa nchi hizo zilishajipatia uhuru wa kiutawala, ugumu ulikuwepo hasa kwenye kutengeneza uhuru wa kiuchumi.
Katika mazingira hayo, upatikanaji wa huduma mathalan za umeme, ilikuwa anasa na wachache waliojiweza ndiyo walionufaika nazo, huku makundi makubwa ya wananchi yakikosa huduma hiyo.
Vibatari na vyanzo vingine vya nishati inayozalisha mwanga, ndivyo vilivyotamalaki na katika nyakati hizo, hakuna aliyefikiri kuhusu athari za matumizi ya nishati hizo.
Lakini, katika kipindi cha miaka 60 baada ya muungano, pande zote za muungano zilianzisha shirika kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya nishati hasa ya umeme kwa wananchi na hapo ndipo nuru ya mafanikio ilipoanza kuangaza.
Kuanzishwa TANESCO, ZECO
Mwaka 1964, Zanzibar ilianzisha Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), huku Tanganyika nayo mwaka huo ikianzisha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) baada ya kuungana kwa mashirika mawili yaliyokuwa yanatoa huduma ya umeme.
Mashirika yaliyoungana wakati huo na kuunda TANESCO ni Shirika la Usambazaji Umeme Tanganyika na Shirika la Uzalishaji Umeme Dar es Salaam (DARESCO).
Maboresho ya huduma yalianza taratibu na ulifika wakati mashirika hayo yalishirikiana kutoa huduma kwa wananchi wa maeneo yao, TANESCO ikiwa ndiyo msambazaji mkubwa wa nishati ya umeme bara na visiwani.
Historia ya sekta ndogo ya umeme Zanzibar
Safari ya upatikanaji wa nishati ya umeme katika eneo la Unguja visiwani humo, ilianza na kiwanda cha Kuchoma Makaa ya Mawe cha mwaka 1908 kilichokuwa chini ya Bodi ya Umeme Zanzibar.
Baadaye mwaka 1954 kukawa na Mitambo ya Umeme wa Moto wa Makaa ya mawe na kisha ilibadilishwa na Mitambo ya mafuta ya Dizeli.
Haikuishia hapo, mwaka 1964 lilianzishwa Shirika la Taifa la Mafuta na Umeme Zanzibar (ZSFPC), kisha mwaka 1980 Kisiwa cha Unguja kiliunganishwa na Tanzania Bara kupitia njia ya Usafirishaji umeme ya Nyambizi ya Kilovoti 132/45MVA (Ras Kiromoni hadi Ras Fumba kilomita 37.145).
Kwa upande wa Pemba, ilianza mwaka 1958 katika eneo la Tibirinzi kilipowekwa kiwanda cha kwanza cha umeme na mwaka 1985 kilianzishwa kituo cha umeme cha wesha (4.5MW).
Lakini mwaka 2010 Pemba iliunganishwa kwenye Gridi ya taifa kupitia Majani Mapana, Tanga kupitia njia ya usafirishaji umeme chini ya bahari ya Kilovoti 33/20MW yenye urefu wa kilomita 75.
Mafanikio TANESCO
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Gissima Nyamo-hanga anaweka wazi mafanikio ya shirika hilo katika safari hiyo ya miaka 60, akaanza kwa kurejea yaliyotokea mwaka 1980.
Katika mwaka huo, Nyamo-hanga anasema kwa mara ya kwanza TANESCO ilijenga njia ya kusafirisha umeme za ardhini, zenye ukubwa wa kilometa 37.14 kutoka Rati kilomoni , Tegeta -Dar es Salaam hadi Rati Fumba visiwani Zanzibar, kiasi cha umeme wa Megawati 45.
“Miaka 43 iliyopita ambayo inakaribia na miaka 60 ya muungano wa Tanzania Bara na visiwani kwa mara ya kwanza tulijenga underground cable ya kusafirisha umeme kutoka Dar es salaam kwenda Zanzibar” anasema.
Baada ya kuongezeka kwa matumizi ya umeme Zanzibar mwaka 2013, mkurugenzi huyo anasema TANESCO ilijenga njia nyingine ya kusafirisha umeme ya ardhini kwenda visiwani humo iliyosafirisha Megawati 100.
“Hizi ndizo njia mbili zinazotumika kupeleka umeme Zanzibar hadi sasa,” anasema Nyamo-hanga.
Si hivyo tu, anasema mwaka 2010 Pemba iliunganishwa na Tanzania bara kupitia eneo la majani mapana mkoani Tanga, kupitia ujenzi wa njia ya umeme ya megawati 20, umbali wa kilometa78 chini ya bahari kufikisha huduma hiyo katika visiwa hivyo.
Anasema njia hiyo hadi sasa inaendelea kutumika kufikisha huduma ya umeme visiwani Pemba.
Ujenzi njia kubwa
Kwa kuwa matumizi ya umeme Zanzibar yanaongezeka kila siku, Mkurugenzi huyo anasema TANESCO inadhamiria kujenga njia kubwa za umeme zitakazokuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kusafirisha nishati hiyo kwenda Zanzibar.
Anasema hatua hiyo inafikiwa ili kuendana na mahitaji ya umeme kwa wananchi wa Unguja na Pemba.
Hata hivyo, juhudi za kuhakikisha umeme unapatikana kwa wananchi baada ya Muungano hazikuwa za awamu moja ya utawala, kila awamu ilitekeleza wajibu huo kufanikisha dhamira.
Na huo ndiyo mzizi wa kupatikana kwa mafanikio lukuki katika usambazaji wa umeme kwa wananchi wa Tanzania kwa ujumla wake.
Matunda ya juhudi za kila awamu ya Serikali, yanashuhudiwa katika awamu ya nane ya Serikali ya Zanzibar chini ya Rais Dk Hussein Ali Mwinyi aliyeamua kupunguza gharama mbalimbali za upatikanaji wa umeme visiwani humo.
“Kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma za umeme kwa urahisi, Serikali imepunguza bei ya kuunganisha umeme kwa wananchi kwa wastani wa asilimia 50.
“Punguzo hilo ni kutoka Sh464,000 hadi Sh200,000 kwa gharama za uungaji usiozidi mita 30. Vile vile, kutoka Sh1.7 milioni hadi Sh690,000 kwa gharama za uungaji wa nguzo moja na kutoka Sh2.6 milioni hadi SH1.04 milioni kwa gharama za uungaji wa nguzo mbili,” anasema Rais Mwinyi alipohutubia taifa mwanzoni mwa mwaka huu.
Kutokana na hatua hiyo, Rais Mwinyi anasema idadi ya wateja wanaoomba kuunganishiwa umeme imeongezeka hadi kufikia wastani wa wateja 200 kwa siku, kutoka wastani wa wateja 50 kwa siku hapo awali.
Kuongezeka kwa mahitaji Pemba, Unguja
Hatua hizo zote zimechagizwa na kuongezeka kwa mahitaji ya umeme katika visiwa hivyo, ambayo kimsingi yametokana na uwepo wa viwanda.
Mathalan, mwaka 2019 mahitaji ya umeme Pemba yalikuwa ni Megawati 10, wakati Unguja ni Megawati 86.
Mwaka 2020 yaliongezeka hadi kufikia megawati 12.8 kwa Pemba, wakati megawati 85.3 kwa upande wa Unguja.
Kwa mwaka 2021 mahitaji yaliongezeka hadi kufikia megawati 12.7 kwa upande wa Pemba, huku Unguja yakifikia megawati 91.4
Ongezeko la mahitaji lilishuhudiwa pia mwaka 2022 na kufikia megawati 13.3 kwa Pemba na megawati 107 kwa Unguja.
Katika mwaka 2023 kiwango cha mahitaji kilifikia megawati 13.7 kwa Pemba, lakini megawati 122.9 kwa Unguja.
Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji, miradi mbalimbali inatarajiwa kujengwa ikiwemo, laini ya kusafirisha kwa njia ya nyambizi 220 yenye uwezo wa kubeba Megawati 240 kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar.
Laini nyingine ni ya Kilovoti 132 ya kusafirisha umeme yenye uwezo wa kubeba megawati 150 kutoka Tanga hadi Pemba, huku njia nyingine mbili zitafuatia njia iliyopo ya nyambizi.
Mafanikio ZECO
Anasema wananchi wengi wamefikiwa na huduma ya umeme ambapo Shirika la ZECO limewaunganishia umeme wananchi 93,124 na kati yao Unguja ni 78,122 na Pemba ni 15,002.
Kwa upande wa nishati vijijini, hadi miaka 60 ya muungano inafikia ZECO ilishasambaza huduma hiyo kwa Vijiji 190 kati ya hivyo, vya Unguja ni 116 na Pemba ni 74, sawa na asilimia 62 ya Vijiji 305 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025.
Ndani ya miaka hiyo 60, Zanzibar imefanya kila namna kuhakikisha inapata vyanzo vyake vya ndani vya uzalishaji umeme na katika kufanikisha hilo, Serikali visiwani humo imesaini mkataba wa mauziano ya umeme (PPA) na Kampuni ya Generation Capital Ltd kwa lengo la kuwekeza katika nishati ya umeme wa jua kwa kujenga mtambo wenye uwezo wa kuzalisha megawati 130.
Kadhalika, Serikali hiyo imetiliana saini na Kampuni ya ESR ya Ujerumani itakayozalisha megawati 15 za umeme wa jua kwa ajili ya kisiwa cha Pemba.
Sambamba na hatua hiyo, Serikali inashirikiana na mshauri elelezi kutoka Kampuni ya Novavis International ya Marekani kufanya upembuzi yakinifu wa kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya umeme mdogo katika baadhi ya maeneo Zanzibar.
Vile vile, mshauri elekezi wa Kampuni ya WSP ya Canada amepatikana kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa mradi wa ujenzi wa laini kubwa ya kilowati 132 ya Mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba kwa ufadhili wa AfDB, KOICA na TANESCO.
Ushirikiano Tanesco, Zeco
Tangu mwaka 1980 wakati kukiwa na njia ya moja ya kusafirisha umeme kutoka kituo kidogo cha Ubungo jijini Dar es Salaam hadi Unguja hadi sasa, TANESCO na ZECO zimekuwa zikishirikiana kuhakikisha Zanzibar inapata umeme wa uhakika kulingana na Dira yake ya 2050.
Hayo ni kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Gissima Nyamo-Hanga alipozungumza kuelekea hafla ya maadhimisho ya mapinduzi ya Zanzibar.
Anasisitiza TANESCO itabaki kuwa mshirika wa kimkakati wa ZECO katika kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa wananchi wa Zanzibar kwa utulivu na ubora ili kusaidia shughuli za kijamii na kiuchumi.
Kadhalika, katika kupigia msumari uimara wa ushirikiano wa mashirika hayo katika utendaji, Wizara ya Nishati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Maji, Nishati na Madini ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zimesaini hati ya makubaliano inayolenga kuimarisha ushirikiano katika maeneo mbalimbali.
Maeneo ya ushirikiano yaliyotiliwa saini ni uandaaji wa sera na sheria, utafiti kuhusu uendelezaji wa sekta ya nishati, kubadilishana takwimu, uzoefu na utaalam katika maeneo yanayohusu sekta.
Hati hiyo ya makubaliano imetiwa saini na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko kwa upande wa Tanzania Bara na Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Zanzibar, Shaib Hassan Kaduara katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam Novemba 12, mwaka 2023.
Kauli za mawaziri
Akizungumza katika hafla hiyo, Dk Biteko anasema kutiwa saini kwa hati hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi ambao mara kadhaa wametoa maelekezo kwa Wizara hizo mbili kuwa na ushirikiano ili kuendeleza Sekta ya Nishati nchini.
“Viongozi wetu wakisema, kinachotakiwa kutokea ni matokeo ya kile kilichosemwa, vinginevyo tutakuwa hatuwasaidii kama wanasema na hakuna mabadiliko, ninataka niwahakikishie kwamba sisi tunathamini sana mashirikiano tuliyonayo na ushirikiano huu utakuwa endelevu,” anasema Dk Biteko.
Kwa mujibu wa Dk Biteko, pamoja na taasisi nyingine, makubaliano hayo yamehusisha Tanesco na Zeco.
“Tumesaini hati hizi si kwa ajili ya kupiga picha bali tunataka tuone matokeo yanatokea, hivyo tukafanye ufuatiliaji wa yale tuliyokubaliana.
“Inabidi tuwe na timu ndogo za kufuatilia yale tuliyokubaliana ili mwisho wa mwaka tupime tumefika wapi. Kwa upande wa Tanzania Bara tutahakikisha kila tulichokubaliana kinatekelezwa,” anasema.
Katika hotuba yake hiyo, Dk Biteko anasisitiza matumizi ya nishati safi ya kupikia sasa hautaishia Tanzania Bara pekee bali hatua za uhamasishaji zitafanyika hadi Zanzibar hivyo Wazanzibar watafaidika pia kwa kupata mitungi ya gesi lengo likiwa ni kuwahamasisha kutumia nishati safi ya kupikia.
Kuhusu umeme, anasema laini ya Kilovoti 132 inayotoa umeme Tanzania Bara kwenda Zanzibar imeshazidiwa kwani matumizi ya umeme yameshakuwa makubwa kutokana na shughuli za utalii, viwanda na matumizi mengine hivyo kwa sasa mpango uliopo ni kujenga laini ya kV 220 ili kupeleka umeme wa uhakika visiwani humo.
Hata hivyo, Dk Biteko anasema makali ya nishati hiyo yanaendelea kupungua, kwani upungufu wa awali wa umeme ulikuwa megawati 810 lakini sasa ymefikia megawati 240 na hivi karibuni yanatarajiwa kuisha.
Kwa upande wake, Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Zanzibar, Shaib Hassan Kaduara anasema hati zilizosainiwa ni nyenzo za kuendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali kwenye sekta ya Nishati.
Anasema matarajio yake ni kwamba wataalamu wa Tanzania Bara na Zanzibar wataendelea kushirikiana kwenye masuala mbalimbali ikiwemo la kutatua changamoto ya upotevu wa umeme unaotokana na wizi au masuala mengine ya kitaalamu. |
Hivi unajua kuwa uwepo wa vivuko viwili vidogo vya kampuni ya Azam Marine ‘Sea Tax 1 na 2’ vinavyovu | Hivi unajua kuwa uwepo wa vivuko viwili vidogo vya kampuni ya Azam Marine ‘Sea Tax 1 na 2’ vinavyovusha abiria Kigamboni, vinaugharimu Wakala wa Huduma za Umeme na Ufundi Tanzania (Temesa) Sh5 milioni kwa siku?
Kwa malipo hayo, Temesa inagharimika kulipa Sh1.8 bilioni kwa mwaka na ndicho kiasi ilichoilipa Azam Marine kutokana na huduma za vivuko hivyo kuanzia Julai 1, 2022 hadi Juni 30, 2023.
Kwa taarifa yako, kiwango hicho cha malipo kiliyoyafanya kwa Azam Marine ni theluthi moja ya mapato yote ya Sh5.76 bilioni yaliyokusanywa na wakala huo kwa kipindi cha Julai 2022 hadi Juni 2023.
Hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere katika ukaguzi wake wa Serikali Kuu wa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2023.
Hatua hiyo kwa mujibu wa Kichere, imeifanya Temesa kubaki na Sh3.93 bilioni kwa ajili ya kugharimia uendeshaji ikiwemo mafuta ya vivuko, gharama za kazi, ukarabati, matengenezo na nyingine.
Hata hivyo, CAG anabainisha kiwango hicho kilichobaki cha Sh3.93 bilioni hakitoshelezi kulipia gharama hizo, hivyo kuisababisha Tesema kutumia fedha za vyanzo vingine kugharamia uendeshaji wa kituo cha Magogoni na Kigamboni.
Mzizi wa ukodishaji huo
Juni 14, mwaka 2022 ndipo Temesa ilipoingia mkataba wa makubaliano na Kampuni ya Azam Marine Ltd kwa ajili ya kukodi na kuendesha vivuko hivyo viwili vya baharini kati ya Magogoni na Kigamboni.
Mpango huo, ulilenga kuongeza uwezo wa Temesa kuhudumia wateja kutokana na ukarabati mkubwa wa Kivuko cha MV Magogoni.
Taarifa ya CAG, ilibainisha kila kivuko kilikuwa na uwezo wa kubeba abiria 250 kwa kila safari, huku kifungu namba 5 cha mikataba wa makubaliano, Temesa inalazimika kuilipa Azam Marine Ltd ada ya huduma kila siku Sh5 milioni pamoja na kodi ya ongezeko la thamani na ya zuio ya asilimia tano.
“Mkodishaji, Kampuni ya Azam Marine Ltd itatoa ankara ya malipo kila mwezi inayoeleza idadi ya siku ambazo huduma ilitolewa kwa mkodishwaji katika mwezi husika,” inaeleza ripoti hiyo.
Mapendekezo ya CAG
Kutokana na mazingira hayo, CAG alisema kuendelea kukodisha vivuko kutoka kwa kampuni hiyo, kunaathiri uendelevu wa huduma ya kivuko katika Kituo cha Magogoni - Kigamboni.
“Hali hii inasabisha Wakala kuendelea kutegemea ruzuku ya Serikali kugharamia shughuli zake badala ya kujitegemea,” alisema.
Alipendekeza Temesa itathmini mikakati mbadala ya kupunguza utegemezi wa vivuko vya mwendokasi vilivyokodishwa, ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vivuko ili kukabiliana na ongezeko la wateja.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mtendaji Mkuu wa Temesa, Lazaro Kilahala alitaka atafutwe mkuu wa mawasiliano wa wakala huo kwa ajili ya ufafanuzi.
Kauli hiyo ya Kilahala imekuja wakati ambao tayari, Mwananchi ilishamtafuta mkuu wa mawasiliano, Alfred Mgweno aliyesema kwa uzito wa jambo hilo lipo nje ya uwezo wake kulizungumzia na alielekeza atafutwe mtendaji mkuu.
Alipotafutwa tena Kilahala kwa njia ya simu, hakupokea na hata ujumbe mfupi hakujibu. |
Uhuru wa biashara, kuishi popote na muingiliano wa watu ni baadhi ya mambo yanayotajwa na wadau kuwa | Uhuru wa biashara, kuishi popote na muingiliano wa watu ni baadhi ya mambo yanayotajwa na wadau kuwa faida za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Faida hizo zinatajwa zikiwa zimesalia siku chache kabla ya Tanzania kuadhimisha miaka 60 ya Muungano, ulioasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa Tanganyika na Abeid Amani Karume kwa upande wa Zanzibar.
Mataifa hayo yaliungana Aprili 26, mwaka 1964 na hadi sasa unafikisha miaka 60, huku wadau mbalimbali wakiwemo wananchi wakisema hatua hiyo imechagiza kupatikana kwa faida lukuki.
Wafanyabiashara
Hanifah Khamis Makame ni mfanyabiashara visiwani humo, anasema ingawa hakuwepo katika visiwa hivyo kabla ya Muungano, zipo faida anazoziona sasa.
Kulingana na mfanyabiashara huyo, kabla ya muungano Zanzibar na Tanganyika zilikuwa nchi mbili tofauti na kwamba ili uingie kwenye moja ya mataifa hayo ilikubidi uwe na pasi ya kusafiria.
Lakini, hatua ya kuungana imerahisisha muingiliano wa watu kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kutanua wigo wa soko na upatikanaji wa bidhaa kwa ajili ya biashara.
“Zanzibar ina watu wachache, fikiria watu milioni tatu ndilo lingekuwa soko la ndani, kwa namna yoyote soko letu lingekuwa dogo. Lakini baada ya Muungano soko limepanuka maana tunauza bara na Zanzibar,” anasema.
Hanifah anasisitiza hata upatikanaji wa bidhaa umerahisishwa na Muungano huo kwa kile anachofafanua kuwa, isingekiuwa rahisi kusafirisha mzigo kutoka Tanzania bara kama lingekuwa taifa linalojitegemea.
“Kwa vyovyote ingekuwa gharama kubwa kusafirisha maana ni kama una export, lakini sasa hivi bidhaa nyingi tunatoa bara kuja kuuza huku Zanzibar,” anaeleza.
Utalii
Mwenyekiti wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar (ZATI), Rahim Bhaloo anasema fukwe za visiwani humo zisingekuwa chochote kama kusingekuwa na mbuga za wanyama ambazo kwa pamoja zinavutia utalii.
Kadhalika, anaeleza hata mbuga za wanyama zilizopo Tanzania bara zisingekuwa chochote kama kusingekuwa na visiwa na fukwe kutoka Zanzibar ambazo kwa pamoja zinatengeneza bidhaa inayovutia utalii zaidi.
Anasema uwepo wa vyanzo hivyo vya utalii ni matokeo ya mataifa hayo kuungana, hivyo vinmeifanya Tanzania iwe na fukwe nzuri, kadhalika mbuga nzuri za wanyama kwa ajili ya soko la utalii.
Faida nyingine ya Muungano wa mataifa hayo kwa mujibu wa Bhaloo ni kubadilishana nguvu kazi katika sekta ya utalii na hivyo kuifanya iwe bora zaidi.
“Ukizingatia kufunguka kwa soko la Zanzibar, kumesaidia watu kutoka bara kupeleka bidhaa zao Zanzibar na wanapata masoko, hii ni faida ya Muungano,” anasema.
Anasisitiza hatua ya Tanzania kuwa na ndege zake ni matokeo ya Muungano uliosababisha kuongezeka kwa soko la abiria na mahitaji ya wasafiri kutoka nje kutembelea nchini kwa sababu za kitalii na mambo mengine.
Anasema kabla ya Muungano hakukuwa na taifa lolote kati ya hayo mawili lililokuwa na shirika lake la ndege na kumiliki ndege, kwa kuwa soko la wasafiri kwa usafiri huo lilikuwa dogo.
Hata hivyo, anaeleza uwepo wa changamoto na mawazo mbadala katika Muungano ni jambo la kawaida na halipaswi kuwa chachu ya pande hizo mbili kutengana.
Mtazamo wa wanazuoni
Mhadhiri wa Rasilimali watu na Utawala wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (Tudarco), Dk Lazaro Swai anasema Muungano huo umekuwa chachu ya utekelezaji wa wazo la umajumui wa Afrika unaotaka waafrika wawe wamoja.
Mbali na hilo, mwanazuoni huyo anaeleza hatua ya Tanganyika na Zanzibar kuungana kumefaidisha pande zote mbili katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali zikiwemo za maendeleo.
Kwa mujibu wa Dk Swai methali ya umoja ni nguvu inasadifu tija ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwani kuungana kwa mataifa hayo kumeyafanya yawe na nguvu ya pamoja.
Anaeleza kile ambacho kilikuwa kikifanywa na watu wachachem baada ya kuungana ameeleza kinafanywa kwa kushirikiana na hivyo kuongeza tija au ufanisi wake.
“Ndiyo maana leo hii unaona Tanzania inakuwa kwa kasi kiuchumi, ni kwa sababu kuna watu kutoka pande mbili wanaoshirikiana katika mambo mbalimbali zikiwemo shughuli za maendeleo na matokeo yanayonekana,” anasema.
Anasema isingekuwa rahisi kwa Tanganyika kuwa katika mahala salama, iwapo kusingekuwa na Muungano kwa kuwa visiwa vya Zanzibar vingeweza kutumika kama njia ya wahalifu.
“Kwa sababu tupo pamoja na tuna nguvu moja, hilo haliwezi kupata nafasi, hizo ndizo faida za muungano,” anasema.
Lakini, anasema uwepo wa Muungano na namna unavyoendelea kudumu unaonyesha uhalisia wa Afrika kwamba inawezekana kuungana, kama ilivyotakiwa na waasisi wa mataifa mbalimbali.
“Muungano huu umekuwa kioo cha kuonyesha kwamba muungano kati ya nchi za kiafrirka inawezekana na huu wa Tanzania ndiyo kielelezo,” anaeleza.
Hoja zilizoibuliwa na Dk Swai zinashabihiana na kilichoelezwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Profesa Francis Matambalya.
Katika hoja zake kuhusu Muungani, Profesa Matambalya anasema faida za muungano hutafsiriwa na falsafa ya umajumui wa Afrika ambao msingi wake ni kuifanya Afrika kuwa jamii moja.
Kwa sababu Afrika haikuwa imeungana tangu awali, mwanazuoni huyo aliyebobea katika biashara za kimataifa, anasema bara hilo limejikuta limegawanyika katika makundi.
Anasema hali ndiyo iliyoifanya Afrika kushindwa katika vita kadhaa dhidi ya watu kutoka nje ya Afrika, kwa kuwa hawakupigana na bara hilo kwa ujumla wake, bali ni vikundi vikundi vilivyokuwa vimegawanyika.
Anafafanua hatua ya waafrika kushindwa kuungana kumesababisha kufuta utambulisho wake katika baadhi ya maeneo na hivyo kulazimika kuiga utambulisho wa wengine.
“Unapopoteza utambulisho wako, utajikuta uafrika wako kwa ujumla unapotea moja kwa moja,” anasema.
Kwa upande wa Tanganyika na Zanzibar, anasema kuungana kwake kumefanya falsafa ya umajumui wa Afrika itekelezeke miongoni mwao.
Pamoja na hilo, anasema angalau zimeonyesha umoja wa waafrika katika muungano huo, kwani hadi sasa pande zote mbili zinashirikiana katika shughuli nmbalimbali.
Anaeleza kilichoyafaidisha mataifa hayo baada ya kuungana ni kutengeneza jamii moja, inayolinda utambulisho wake.
Umuhimu wa umoja huo, anasema umeshuhudiwa kupitia matukio kadhaa likiwemo la kupigwa kwa watu waliodaiwa kula wakati wa mwezi mtukifu wa Ramadhan.
Profesa Matambalya anasisitiza kilichofanya Serikali ya visiwani humo itoe tamko kuhusu kupigwa kwa watu hao ni umoja uliokuwepo miongoni mwa mataifa hayo.
Faida nyingine, anasema ni uhuru wa kutembea na kuishi kutoka eneo moja kwenda lingine.
Kwa mujibu wa mwanazuoni huyo, mwaka 2019 kulikuwa na Wazanzibari 700,000 wanaoishi Tanzania bara, akifafanua uhuru huo ni matunda ya Muungano.
Lakini hata biashara, anasema mtu anayetoka Tanzania bara ana nafasi ya kwenda Zanzibar kufanya biashara zake bila kughudha, tofauti na iwapo nchi hizo zisingeungana. |
Wakati baadhi ya taasisi za Serikali zikilia uhaba wa bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya k | Wakati baadhi ya taasisi za Serikali zikilia uhaba wa bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kipaumbele, imebainika Sh4.05 bilioni zipo mifukoni mwa baadhi ya mashirika kwa miaka saba bila kutumika.
Kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere, fedha hizo zipo katika akaunti za benki za taasisi sita za Serikali tangu mwaka 2018.
Fedha hizo zipo katika akaunti za Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mfuko wa Tuzo na Tozo wa Jeshi la Polisi, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Sanaa Utamaduni na Michezo na Hospitali ya Sekou-Toure.
Ripoti hiyo iliyowasilishwa bungeni jijini Dodoma jana na Kichere, imebainisha mchaganuo wa fedha hizo kwa kila taasisi.
Ukaguzi wa Kichere, umeweka wazi Wakala wa Ndege za Serikali ina Sh2.11 bilioni, fedha ambazo ni fidia ya athari ya kufilisika ya kampuni ya M/S C-Series zilizozuiwa tangu mwaka 2018 hadi 2022.
Kuzuiwa huko, kumetokana na kile kilichoelezwa katika ripoti hiyo kuwa, kampuni hiyo ilishindwa kuwasilisha ndege iliyonunuliwa kulingana na makubaliano ya ratiba.
Mfuko wa Tuzo na Tozo wa Jeshi la Polisi, ripoti hiyo imesema una Sh148.24 milioni na zilipelekwa kimakosa katika mfuko huo.
"Fedha hizo zilipaswa kupelekwa katika akaunti ya makusanyo ya Jeshi la Polisi tangu mwaka 2019," amesema Kichere kupitia ripoti hiyo.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Kamishna wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi Tanzania, Liberatus Sabas amesema ni mamlaka ya Msemaji wa Jeshi hilo, David Missime kuzungumzia hilo.
Hata hivyo, alipotafutwa mara kadhaa, Misime simu yake iliita bila majibu.
Wizara ya Uchukuzi nayo, imebaki na Sh409.7 milioni zilizohifadhiwa tangu mwaka 2021 hadi 2023 katika akaunti ya amana bila kutumika, kulingana na CAG.
Pamoja na wizara hiyo, Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo ina Sh390.25 milioni ambazo ni fedha za zuio kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa Benjamin Mkapa zilizohifadhiwa katika akaunti ya amana kwa zaidi ya miaka mitano.
Kwa upande wa Hospitali ya Sekou-Toure, CAG amesema imehifadhi Sh1 bilioni zilizotolewa tangu Novemba 10, 2022 kwa ajili ya ukarabati ya majengo, lakini hazijatumika na zimehifadhiwa katika akaunti ya amana.
Kutokana na mazingira hayo, Kichere amependekeza Serikali itoe idhini ya matumizi kwa fedha zilizokaa muda mrefu bila kutumika ili zitumike kwa shughuli za maendeleo zilizopangwa.
"Aidha taasisi zote zihakikishe makusanyo yote yanawasilishwa katika mfuko mkuu ili kutekeleza vipaumbele vya kibajeti," amesema. |
Kikiendelea kufanya siasa zake kisasa na kutanua wigo wa kusajili wanachama na wafuasi kwenye maeneo | Kikiendelea kufanya siasa zake kisasa na kutanua wigo wa kusajili wanachama na wafuasi kwenye maeneo mbalimbali nchini, Chama cha ACT Wazalendo kitavamia mkoa wa Kilimanjaro ambao kwa muda mrefu umekuwa ukiaminika kuwa ngome ya Chadema, kufanya uzinduzi wa kishindo kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake.
Chama hicho kilichojipambanua kufanya siasa za kupigania maslahi ya wote na Zanzibar yenye mamlaka kamili, kinatimiza muongo mmoja, kikiwa kimevuka viunzi kadhaa katika safari ya uhai wake.
ACT Wazalendo inatimiza umri huo katika kipindi ambacho, muasisi wake, Zitto Kabwe tayari ameng’atuka katika uongozi wa chama hicho, baada ya kuhudumu kwa miaka 10 tangu kilipoanzishwa.
Mikoba ya Kabwe imerithiwa na Dorothy Semu, anayeandika historia ya kuwa mwanamke wa pili kushika uongozi wa juu wa chama cha siasa, baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.
Taarifa kuhusu uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 10 ya chama hicho, ilitolewa jana na Naibu Katibu wake wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma, Shangwe Ayo.
Kulingana na Shangwe, Kilimanjaro ni moja ya Mikoa ambayo chama hicho kitafanya mkutano wa kidemokrasia, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho hayo.
Mkutano huo, utakaofanyika Aprili 27, mwaka huu, kwa mujibu wa taarifa hiyo, wanachama wote wa chama hicho watakutana na Kiongozi wao, Dorothy Semu kujadiliana naye masuala mbalimbali.
“Katika Mkutano huo wa Kidemokrasia Nembo mpya ya chama na Bendera mpya vitazinduliwa rasmi. Mkutano wa Kidemokrasia ni Kikao cha kikatiba na cha wazi kwa wanachama wote watakaokuwa na uwezo wa kufika Moshi,” alisema.
Hata hivyo, alisema chama hicho kitaweka utaratibu wa kufanikisha wanaotaka kuhudhuria mkutano huo Moshi, Kilimanjaro.
Kabla ya Kilimanjaro, Shangwe alisema maadhimisho hayo yataanzia Aprili 21, visiwani Zanzibar litakakofanyika kongamano la vijana.
“Kongamano hili litafanyika Unguja na kuhudhuriwa na mamia ya Vijana wa Zanzibar na viongozi wa Kitaifa wa chama na wadau mbalimbali wa mageuzi nchini,” alisema.
Alieleza mkesha wa maadhimisho hayo unatarajiwa kufanyikaMei 4, mwaka huu Makao Makuu ya chama hicho katikia Jengo la Maalim Seif, Magomeni Dar es Salaam na Ofisi Kuu ya chama hicho Vuga Zanzibar.
Kilele cha maadhimisho hayo, alisema itakuwa Mei 5, mwaka huu katika Viwanja vya Mwami Ruyagwa, Kata ya Gungu Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma.
Kulingana na Shangwe, kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni ‘Miaka 10 ya kupigania maslahi ya wote na Zanzibar yenye mamlaka kamili.’
Maadhimisho hayo, alisema yataambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo vikundi vya wanawake na vijana wa chama hicho kutoa misaada kwa jamii, ikiwemo kwa wahanga wa Rufiji mkoani Pwani.
“Pamoja na ushiriki huu wa mikutano na makongamano wanachama wa ACT Wazalendo watashiriki shughuli mbalimbali za kijamii kama vile kuchangia damu katika Benki ya Damu ya Taifa, kufanya usafi kwenye masoko, kufanya usafi kwenye hospitali na kuwafariji wagonjwa waliolazwa katika hospitali hizo,” alisema.
Akizungumzia miaka 10 ya chama hicho, mwanazuoni wa sayansi ya siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Matrona Kabyemela alisema ACT Wazalendo ni moja ya vyama vinavyoonyesha kukua kwa kasi.
Alisema mara nyingi vinapoanzishwa vyama vya siasa, watu hutarajia kufa kwake, lakini chama mwenendo wa chama hicho umekitofautisha na vingine.
Lakini, alieleza uongozi makini na mikakati ya endelevu ya uendeshaji ndiyo msingi wa uhai wake, akisisitiza kuna taswira ya kukua zaidi baada ya miaka 10 ijayo.
“Kama tunavyojua kwa sasa ndiyo chama kikuu cha upinzania kwa upande wa Zanzibar na kipo ndani ya Serikali kwa sasa. Kwa upande wa bara bado lakini kinaonyesha nguvu kubwa,” alisema.
Hata hivyo, alisisitiza hatua ya kuendana na siasa za wakati ni jambo lingine linalodumisha uhai wa chama hicho, akifafanua kimewekeza kwa vijana wenye taaluma na kinawatumia ipasavyo.
Kwa mujibu wa Dk Kabyemela hatua ya kufanya maadhimisho ni jambo sahihi hasa ukizingatia, Tanzania inakaribia kwenye chaguzi, hivyo kinajenga ushawishi kwa wananchi. |
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere imebaini mambo manne | Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere imebaini mambo manne, ikiwa ni changamoto katika ufanisi wa utendaji ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).
Kulingana na hoja za Kichere katika ripoti hiyo, kati ya mambo hayo yapo yanayoliacha shirika hilo katika madeni, mgogoro na washirika wake, lakini mengine yanalisababishia hasara.
Pamoja na hoja hizo za CAG, shirika hilo limesema linachokifanya ni kuandaa majibu juu ya yote yaliyobainishwa katika ripoti hiyo na kuyawasilisha kama inavyopaswa.
“Hizo zote zilizotolewa ni hoja za CAG na sisi kama shirika tunaziandalia majibu, hicho ndicho nachoweza kukwambia kwa sasa,” alisema Kenneth Boymanda, msemaji wa Tanesco.
Hoja za CAG
Uchambuzi wa Kichere katika ripoti yake ya ufanisi wa mashirika ya umma ya mwaka wa fedha unaoishia Juni 2023, shirika hilo linakabiliwa na deni la Sh240.28 bilioni kutoka kwa makandarasi na malipo ya awali ya fidia.
Deni hilo, kwa mujibu wa ripoti hiyo limetokea katika utekelezaji wa mradi wa uimarishaji wa gridi ya taifa, ambao jumla ya malipo kwa ajili ya makandarasi na fidia ni Sh331.19 bilioni.
Kati ya fedha hizo, Kichere anasema ni Sh90.91 pekee ndizo zilizolipwa na Tanesco kwa makandarasi na fidia hadi Juni 30, mwaka 2023.
Lakini kilichosababisha kuchelewa kwa malipo hayo, ripoti hiyo inasema ni kukosekana kwa fedha zilizopaswa kutolewa na Wizara ya Nishati ambayo hadi muda huo haikuwa imetoa.
Pamoja na deni hilo, ripoti hiyo inaweka wazi juu ya Sh11.43 bilioni za fidia walizopaswa kulipwa watu wanaoathirika na utekelezwaji wa mradi huo.
Ukaguzi wa CAG ulibini, pamoja na kuidhinishwa kwa tathmini ya fidia, hadi Juni 30 mwaka 2023 malipo hayo hayakufanyika.
“Hali hii inaweza kusababisha mkandarasi kuchelewa kukamilisha mradi kwa wakati kutokana na matatizo ya kifedha yanayosababishwa na ucheleweshaji wa malipo,” alisema.
Alipendekeza Wizara ya Fedha kuhakikisha inatoa fedha hizo ili waathirika wote walipwe stahiki zao kuwezesha utekelezaji.
Mgogoro Tanesco Songas
Ukaguzi wa CAG umebaini kuwepo kwa mzozo kati ya Tanesco na Songas Limited, uliosababishwa na shirika hilo kupinga kufanya malipo ya ununuzi wa umeme yanayofikia Sh67.9 bilioni.
Licha ya Tanesco kuchukua uamuzi huo, Songas imeendelea kujumuisha gharama za kuboresha visima vya gesi katika Ankara za kila mwezi kuanzia Agosti 2022 hadi Juni 2023, zenye thamani ya shilingi bilioni 29.34.
Mzozo zaidi uliibuka Songas ilipotoa ankara nyingine Januari 4 2023, yenye thamani ya Sh23.94 bilioni na dola za Marekani 4.02 milioni.
Hata hivyo, mzozo huo unahusisha deni la kodi ya ongezeko la thamani la Sh11.78 bilioni ambalo halijalipwa kwa Mamlaka ya mapato (TRA) kutokana na kukosekana kwa nyaraka za kuthibitisha.
Hata hivyo, hadi Desemba 2023, suala hilo halikuwa limetatuliwa.
“Kwa kuzingatia muda wa miaka 20 wa mkataba wa ununuzi wa umeme ambao unatarajia kuisha Oktoba 2024 na kuwepo kwa uwezekano wa kuongeza muda.
“Migogoro hii isiposuluhishwa inaweza kuleta utata wakati muda wa mkataba huo utakapoisha na kusababisha kuongezwa kwa muda wa mkataba huo ili kutoa njia ya kusuluhisha mizozo hiyo,” imeeleza ripoti hiyo.
Kwa mujibu wa CAG, Tanesco inapaswa kuishirikisha ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kupitia vipengele vya mikataba au makubaliano vinavyoipa Kampuni ya Songas haki ya kutoza gharama za “sinking” na kutatua migogoro kulingana na masharti ya mikataba.
Mabadiliko mita kabla ya muda
Ukaguzi huo kwa mujibu wa Kichere, umebaini shirika hilo lilifanyia mabadiliko mita za umeme 108,088 kabla ya muda wake wa matumizi kuisha.
Mita hizo ni kati ya 602,269 zilizobadilishwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/23, huku kati ya hizo 13,493 zikibadilishwa ndani ya kipindi cha mwaka mmoja baada ya kufungwa.
Hata hivyo, mabadiliko hayo yamefanyika katika kipindi kifupi cha kati ya mwaka mmoja hadi 15, ilhali muda unaotarajiwa wa matumizi ya mita hizo kabla ya kubadilishwa ni miaka 20.
“Hii imesababishwa na ubora duni wa mita zilizowekwa na mabadiliko ya haraka ya teknolojia yaliyosababisha kushindwa kufikia muda wake uliotarajiwa,” ilieleza ripoti hiyo.
Hata hivyo, CAG katika ripoti hiyo anaeleza kubadilisha mita mapema husababisha gharama zaidi ambayo inaathiri utendaji wa kifedha wa shirika.
“Ninapendekeza Tanesco ichunguze sababu za kubadilisha mita mapema kuliko muda unaotarajiwa wa matumizi, ihakikishe vipimo vya ubora wa mita vinafanyika ili kuongeza ufanisi wa kufikia muda wa matumizi unaotarajiwa ili kupunguza gharama zinazotokana na kubadilisha mita,” alisema.
Malipo holela
Kulingana na ripoti hiyo, katika mwaka wa fedha 2022/23, Tanesco ililipa dola za Marekani 10.16 milioni kwa mzabuni katika mkataba Na. PA/001/2018-2019/HQ/W/31 kwa ajili ya kubunifu, kusimika, kutekeleza, kutoa mafunzo na kuzindua mfumo wa usimamiziwa biashara, kusaidia miundombinu katika mfumo huo na kutoa ushauri elekezi.
“Nilibaini malipo hayo yalifanywa bila kuthibitishwa kwa ubora wa kazi husika na mshauri elekezi,” alisema Kichere.
Hali hiyo, alisema imetokana na mratibu wa mradi aliyeteuliwa kutekeleza majukumu mawili kwa wakati mmoja, kama Meneja wa Mradi na kama mthibitishaji wa malipo ikiwa Mshauri elekezi hayupo.
Katika hali hiyo, alisema kuna hatari ya mzabuni kulipwa kwa kazi zisizotekelezwa kama inavyotakiwa kwenye mkataba. |
Chama cha Wananchi (CUF) kimebaki kuwa miongoni mwa taasisi zilizopata hati yenye shaka kwa mujibu w | Chama cha Wananchi (CUF) kimebaki kuwa miongoni mwa taasisi zilizopata hati yenye shaka kwa mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Hii ni mara ya pili kwa chama hicho kuangukia kwenye orodha hiyo, baada ya ukaguzi wa CAG mwaka jana kukipa chama hicho hati yenye shaka.
Ukiachana na CUF, vyama vingine vilivyoangukia katika hali viliyokuwanayo katika ripoti ya mwaka jana ni NRA, kilichopata hati mbaya, huku AFP CAG akishindwa kukitolea maoni.
Taarifa hizo ni kulingana na ripoti ya ukaguzi wa taarifa za fedha za Serikali Kuu kwa mwaka wa Fedha ulioishia Juni 30, mwaka jana.
CUF
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hati yenye shaka ya chama cha CUF imetokana na taarifa zake za fedha kutojumuisha baadhi ya mali za chama hicho.
“Taarifa ilionesha tu kuwa Chama kinamiliki mali lakini thamani ya mali hizo haikujumuishwa katika taarifa za fedha.
“Jambo hili ni kinyume na matakwa ya aya ya 26 na 27 ya IPSAS 17 (Viwango vya Kimataifa vya Uandaaji wa Hesabu katika Taasisi za Umma) na kanuni ya 22(1) ya Kanuni za Uandaaji wa Taarifa za Fedha za Vyama vya Siasa za Mwaka 2019,” imeeleza ripoti hiyo.
Kutokana na mazingira hayo, ukaguzi wa CAG umebaini thamani ya mali zilizooneshwa katika taarifa za fedha CUF hazikuonesha uhalisia wa mali zake zote.
Akizungumzia hali hiyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano
NRA
Kwa upande wa chama cha NRA ambacho kwa mujibu wa ripoti hiyo CAG kimepata hati mbaya, sababu ni taarifa zake kujumuisha madeni ya Sh2 milioni na hayakuwa na nyaraka toshelezi za kuthibitisha usahihi wake.
Kadhalika, CAG katika ripoti hiyo anasema taarifa ya mizania ya chama hicho ilionesha kuongezeka kwa wadaiwa wake kwa Sh3.75 milioni.
Hata hivyo, imeeleza ongezeko hilo halikuoneshwa katika taarifa ya mapato na matumizi ya chama hicho.
“Taarifa ya mtiririko wa fedha haukuwa na taarifa lingalishi za mwaka wa fedha 2021/22. Kulikuwa na kutolingana kwa taarifa za fedha katika sehemu tofauti za taarifa za fedha, kama vile Taarifa ya Ulinganisho wa Bajeti na Fedha Halisi ilionesha jumla ya fedha iliyopokelewa ya Sh6.03 milioni badala ya Sh2.28 milioni iliyoonekana katika taarifa za mtiririko wa fedha,” ilieleza ripoti hiyo.
AFP
Chama cha AFP nacho hakikubaki salama, katika ukaguzi huo, CAG ameshindwa kutoa maoni kwa sababu taarifa za fedha kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2023 zilizoandaliwa hazikujumuisha taarifa linganifu za mwaka wa fedha uliopita.
“Kutojumuisha taarifa hizi linganifu kuliathiri kwa kiasi kikubwa mawanda ya ukaguzi wa taarifa za fedha za Chama cha AAFP,” imeeleza.
“Upatikanaji wa taarifa hizi ni muhimu kwa sababu zina mchango wa moja kwa moja kwenye usahihi wa taarifa za fedha za mwaka ulioishia Juni 30 2023,” imeeleza ripoti hiyo.
Katika ripoti hiyo, CAG Charles Kichere anasema kutojumuisha taarifa lingalishi kunaathiri kiwango cha kueleweka kwa taarifa hizo na hakumpi mtumiaji taarifa za kutosha ili kumsaidia kufanya maamuzi sahihi.
“Hii imetokana na kuwa taarifa za msingi katika taarifa za mwaka wa fedha uliopita hazikuwasilishwa kwa ajili ya Ukaguzi,” amesema. |
Hivi unajua kuwa asilimia 71 ya Wazanzibari wanaishi kwenye maeneo wasiyoyamiliki? Jambo hilo linata | Hivi unajua kuwa asilimia 71 ya Wazanzibari wanaishi kwenye maeneo wasiyoyamiliki? Jambo hilo linatajwa kukwaza upatikanaji wa fursa zikiwemo za mikopo kwa wananchi hao.
Hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya Finscope Zanzibar ya mwaka 2023, inayoeleza sababu za hali hiyo ni uwepo wa majengo mengi ya kale ambayo mara nyingi ni vigumu mtu binafsi kuyamiliki.
Kulingana na ripoti hiyo, ni asilimia 29 pekee ya wananchi visiwani humo, ndiyo wanaomiliki maeneo wanayoishi na kati yao, asilimia nne wanamiliki kwa ushirikiano.
Pamoja na hali hiyo, ripoti inaeleza asilimia 39 ya wakazi hao wanatamani kumiliki nyumba lakini hawana uwezo huku asilimia 12 wakitamani kumiliki ardhi au shamba.
Si hao pekee, ipo asilimia 13 ya Wazanzibari wenye kiu ya kumiliki biashara baadaye, lakini fedha ndiyo kikwazo na asilimia tatu wanatamani kumiliki mifugo.
Asilimia 12 wanatamani kumiliki gari au vyombo vya moto na asilimia 10 hawajawahi kufikiria juu ya umiliki wa kitu chochote.
Akizungumzia umiliki hafifu wa makazi na ardhi visiwani humo, Mchambuzi wa masuala ya Uchumi na biashara, Oscar Mkude amesema hali hiyo inawafanya wananchi kushindwa kufikia fursa mbalimbali ikiwemo mikopo.
“Kuna mikopo inatolewa kwenye taasisi za fedha, ukiwa na ardhi unaweza kupewa, mikopo hiyo ndiyo hutumika katika shughuli mbalimbali za kujiendeleza kiuchumi ambazo hufanywa na watu,” amesema Mkude.
Kadhalika, amesema hali hiyo inawafanya wananchi kuwa kama wakimbizi katika eneo walikozaliwa na hivyo kuwapa mazingira magumu ya kufanya shughuli za biashara.
Hata hivyo, Mkude amesema kwa Zanzibar kutomiliki ardhi linaweza lisiwe jambo la ajabu kwa kuwa maeneo mengi yana majengo ya kale ambayo ni vugumu kwa mtu binafsi kuyamiliki.
Kauli hiyo inathibitishwa na ripoti hiyo, inayotaja baadhi ya maeneo kuwa na umiliki kidogo ukilinganisha na mengine.
Kaskazini Unguja ndiyo inayoongoza kwa asilimia 43 ya wakazi kumiliki ardhi wanayoishi, Kusini Unguja asilimia 32, Mjini Magharibi asilimia 25, Kaskazini Pemba asilimia 30, Kusini Pemba asilimia 23.
“Wakati mwingine pia ‘sample’ iliyotumika katika utafiti inaweza isitoe majibu yenye mashiko kama Zanzibar ina watu zaidi ya milioni tatu kwa mujibu wa Sensa ikatumika sample ya watu 300,000 lazima tutapata matokeo dhaifu,” amesema Mkude.
Wakati yeye akiyasema hayo, Mtaalamu wa Uchumi Profesa Aurelia Kamuzora amesema shughuli za upangaji miji zinaweza kuwa kikwaza cha umiliki.
Aliijenga hoja hiyo kwa kutolea mfano hasa wa maeneo ya vijijini, ambayo mara nyingi hayapimwi na kusababisha umiliki kuwa hafifu.
Kauli ya Serikali
Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar, Rahma Kassim Ali alisema yapo maeneo ambayo hayana matatizo na si yaliyopangwa kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi watu wanayoweza kumiliki.
Mbali na kumiliki pia alisema ni vyema watu kuhakikisha wanapitia michakato yote inayotakiwa ikiwemo kutafuta hati za umiliki ili kuweka uhalali.
“Hapa kwenye hati ndiyo kuna tatizo, elimu bado iko chini, watu wanazitafuta wanapokuwa na shida ya mikopo ndiyo wanaanza kuhangaika sasa suala linalohusu ardhi si kitu cha siku moja inachukua muda na wakati mwingine hadi wiki tatu,” amesema
Moja ya changamoto inayosababisha watu washindwe kurasimisha ardhi zao ni uwepo wa tozo na hata hivyo Serikali inafanyia kazi.
“Zipo kanuni ambazo zinaandaliwa kwa sasa zitakazoshusha tozo hizi ili wananchi waje kufanya uhamishaji wa umiliki kutoka kwa watu waliowauzia kuja kwao, wengi wamekuwa wakija kuomba kufanya hivyo lakini wakiambiwa gharama hawarudi,” amesema.
Gharama hizo, amesema zimekuwa zikitozwa kulingana na ukubwa wa ardhi inayotaka kumilikiwa.
“Lengo la Serikali ya Zanzibar ni kuhakikisha ardhi yote inapimwa, kwa sababu faida ya kuwa na hati ni kupunguza uvamizi wa maeneo,” amesema.
Alitumia nafasi hiyo kuwataka watu waliobadili matumizi ya maeneo kutoka yale yaliyopangwa na kuyafanya makazi, wafuate utaratibu wa kisheria. |
Kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda juu ya uwepo wa watu wakiwemo mawaziri wanaotuma watu | Kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda juu ya uwepo wa watu wakiwemo mawaziri wanaotuma watu kumtukana Rais Samia Suluhu Hassan imezua mjadala, huku ikigawa mtazamo wa Watanzania katika makundi manne.
Katika makundi hayo, wapo wanaoitazama kauli hiyo kama taarifa nyeti na haipaswi kupuuzwa na vyombo vya ulinzi na usalama, lakini wengine wanamkosoa aliyeitoa kwa hoja kuwa, jukwaa alilolitumia si sahihi kutoa taarifa hiyo.
Kundi lingine linahoji iwapo Makonda ana mamlaka ya kisheria ya kutoa taarifa hiyo, kadhalika wapo waliokwenda mbali zaidi wakisema tuhuma zilizotolewa na mkuu huyo wa mkoa dhidi ya mawaziri zinaliweka baraza la mawaziri katika mashaka.
Mzizi wa mitazamo hiyo ni kilichosemwa na Makonda Aprili 12, mwaka huu, alipohutubia katika hafla ya kumbukizi ya miaka 40 ya Hayati Edward Sokoine mkoani Arusha.
Pamoja na mambo mengine, mwanasiasa huyo alitumia jukwaa hilo, kumweleza Rais Samia aliyekuwa mgeni rasmi juu ya uwepo wa watu wakiwemo mawaziri wanaolipa na kutuma watu wamtukane rais mitandaoni.
“Nitumie fursa hii kuwaambia, hasa kaka zangu mnaotuma watu na kulipa kumchokoza mama yangu, ninawajua na mimi mnanijua, narudia, hasa kaka zangu mnaotuma na kulipa watu kumchokoza mama yangu Samia, mnanijua na ninyi nawajua,” alisema Makonda.
Hakuishia hapo, mkuu huyo wa Mkoa aliahidi kuweka hadharani majina ya watu hao iwapo vitendo vya matusi dhidi ya Rais Samia visingekoma kuanzia siku hiyo.
“Na leo (Aprili 12) nataka iwe mwisho kutuma watu wao wanaokutukana kwenye mitandao ya kijamii, Jumatatu (leo) ikiendelea nakutajia majina, wengine ni mawaziri,” alisema.
Kauli na ahadi hiyo ya Makonda, imezua mjadala katika mitandao ya kijamii, wakiwemo wanaomuunga mkono kwa kutoa ahadi za kumlinda Rais Samia dhidi ya watu hao, huku wengine wakimpinga.
Miongoni mwa waliojitokeza kuunga mkono ni Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba aliyetumia kurasa zake za mitandao ya kijamii, kuchapisha picha ya Rais akiwa pamoja naye na kuandika maneno ya kupongeza kazi anayoifanya na kuahidi kumlinda.
Katika chapisho lake hiyo, Dk Nemba aliandika: “Hawakujua utafanya mambo makubwa yote haya, umekamilisha miradi hata iliyoshindikana, umetekeleza miradi kila kata ya nchi hii, umewapa uhuru raia, vyombo vya habari na online media zote za kijamii.
“Unawasomesha watoto wao chekechea mpaka vyuo vikuu, barabara kila kijiji, sekta za uzalishaji zote umeziongezea fedha, umefufua uchumi, umeifungua nchi, umejijengea heshima Duniani kote,” aliandika.
Kulingana na chapisho lake hilo, pamoja na yote yaliyofanywa na mkuu huyo wa nchi, watu hao hawakutaka kuyaona na kwamba wanafanya hivyo kwa makusudi.
“Lakini, hawajataka kuona mazuri yote haya na mengine, sio kwa bahati mbaya, tulijua kuwa kutakuwepo na njama za kukuchafua sana mwaka 2024 na 2025, Tunajua kwenye mikakati yao bado watakuja na mengine ya uongouongo hivi hivi.
“Hatutakubali kuyumbishwa, tutapambana na wanaotumwa na wanaowatuma,” aliandika katika chapisho lake hilo.
Taarifa isipuuzwe
Kwa mtazamo wa Mbunge wa Mvumi (CCM), Livingstone Lusinde taarifa iliyotolewa na Makonda haipaswi kupuuzwa hasa na vyombo vya ulinzi na usalama.
"Nina uhakika vyombo vimesikia na ulivyoona Rais alivyoipokea hiyo taarifa haikumshtua sana kwa sababu anayesemwa vibaya ni Rais na Rais ni taasisi sio Rais Samia. Kwa hiyo kwa sababu taasisi ndio inasemwa vibaya natarajia vyombo vitachukua hatua za haraka," alisema.
Hata hivyo, mbunge huyo alisema uhakika wa uwepo wa mawaziri wanaofanya hivyo au kutokuwepo kwao, utatokana na uchunguzi.
"Kwa hiyo kama mjumbe wa NEC (Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM) na mbunge ninavitaka vyombo vya dola kuchunguza jambo hilo kwa sababu imetolewa na mtu mzito ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha na vile vile ni mteule wa Rais," alisema.
Kauli hiyo ya Makonda imekuwa vigumu kuzungumziwa na Mbunge wa Kasulu Vijijini (CCM), Augustino Vuma aliyesema mkuu huyo wa mkoa ndiye anayepaswa kueleza zaidi.
Pamoja na kujiweka kando huko, mbunge huyo alilaani vitendo vinavyoendelea katika mitandao ya kijamii dhidi ya Rais Samia.
Hata hivyo, alihusisha vitendo hivyo na rasharasha za kuelekea uchaguzi, nyakati ambazo amesema aghalabu fitina hushamiri.
Haikutolewa eneo sahihi
Lakini wapo wanaokosoa hatua ya Makonda kutumia jukwaa hilo kutoa taarifa hiyo, wakisema hapakuwa mahala sahihi kuzungumzwa hayo kama inavyofafanuliwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Karambo mkoani Rukwa, Vitus Nandi.
"Unaposema jambo uwe na uhakika, huenda mwenzetu ana uhakika, lakini sio pale hadharani kwa sababu CCM tuna utaratibu wetu. Hali hii itasababisha athari ndani ya CCM ikiwamo kuwepo kwa makundi ya baadhi ya watu.
"Angefikisha ujumbe kimyakimya maana hii itampunguzia uaminifu, ingawa ametumia haki yake ya kusema ukweli daima, lakini sio kwa njia aliyoitumia," alisema, mwenyekiti wa CCM wilayani Kalambo mkoani Rukwa,” alisema.
Wakati Nandi akieleza hayo, mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa katika Mkoa huo, Yasin Ismail alisema kulipaswa kutafutwa njia mbadala ya kufikisha taarifa badala ya kumwaga mchele hadharani.
Kufanya hivyo, alisema kumewapa ajenda wanasiasa wa vyama vya upinzani.
"Mwenezi wa zamani wa CCM naye ni binadamu, inawezekana alikuwa na nia njema lakini ulimi ulimteleza kwa kufikisha ujumbe wake haraka kwa njia ile. Inawezekana ana ushahidi wa kutosha kwa sababu ana uzoefu kwenye uongozi," alisema Ismail.
Hoja za makada hao, zinawekewa msisitizo na Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, (THRDC), Onesmo Olengurumwa aliyesema zilipaswa kutumika taratibu nyingine kutoa taarifa hiyo na si mbele ya watu wengine.
Katika kauli yake hiyo alisema taarifa hizo zilipaswa kutolewa ndani kwa ndani kwa kuwa zina hatari ya kusababisha mgawanyiko kwa viongozi.
“Mkanganyiko huu unaweza kuchelewa shughuli mbalimbali za kimaendeleo, badala ya viongozi kushirikiana kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleowanakuwa na migongano,” alisema.
Ana mamlaka ya kusema hilo?
Kauli hiyo imeibua hoja juu ya Makonda kuwa na mamlaka ya kuitoa, kama inavyoelezwa na Mchambuzi wa siasa Dk Paul Luisulie.
Alisema mamlaka ya kutoa taarifa kama hiyo ni ya vyombo vya ulinzi na usalama.
“Lakini upande mwingine kauli ile inaleta mgawanyiko mkubwa ndani ya serikali kuwa sasa watu watakuwa wanatuhumiana, mambo mengine ni kuonyana ndani kwa ndani, jambo hili likija katika macho ya umma huwezi kuzuia tafsiri mbalimbali,” Dk Luisulie.
Alisema kauli hiyo pia inajenga kutoaminiana na hata Rais atakuwa na sauti kichwani inayomuambia kuwa kuna watu wanalipa watu ili watukanwe n ahata mawaziri watakosa kujiamini.
Baraza mawaziri shakani
Makamu Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, Joseph Selasini alisema tuhuma hizo dhidi ya mawaziri zinaliweka baraza la mawaziri katika mashaka.
“Lakini ajabu ni kuwa Makonda anao uwezo wa kumfikia Rais sehemu yoyote, kwanini avumilie Rais aendelee kutukanwa hadi apate wasaa wa kuzungumza mbele ya watu vile. Nini kilimfanya Makonda asichukue hatua mapema hadi azungumze sehemu kama ile,” alisema Selasin.
Naibu Mwenezi wa Chama cha ACT Wazalendo, Shangwe Ayo alisema kwa sababu Rais ndiyo Mwenyekiti wa baraza la mawaziri kauli ya Makonda inaonyesha kuwa Rais Samia hufanya kazi na watu wanaomlia njama.
“Hiyo inatoa picha kuwa umefika muda wa Chama cha Mapinduzi kuondoka madarakani kikae chama kingine kinachoweza kuongoza,” alisema Ayo.
Katibu Mkuu wa chama cha UDP, Saumu Rashid alisema jambo hilo ni tuhuma na anayepaswa kuzungumzia ni vyombo vya ulinzi na usalama.
“Lakini amesema Makonda ambaye si hata msemaji wa chama halina uzito, Makonda ni vitu vingi anaongea ukichukulia kila kitu kwa uzito wake na kulikuza inaweza kuchangia kuharibu nchi,” alisema Saumu.
Akitoa mtazamo wa kisheria, Wakili Dominic Ndunguru alisema inakuwa vigumu kumtia mtu hatiani juu ya kauli yake ikiwa hakutaja jina la mtu.
“Mtu akisema baadhi ya watu mtu akisema amshataki itakuwa ni ngumu kwa sababu hakuna mhusika aliyeguswa sasa kwa kile alichokisema Makonda labda tusubiri mpaka Jumatatu,” alisema Ndunguru.
Alisema wakati mwingine kauli kama hizo zinaweza kuwa za kisiasa kuendana na mazingira ambayo kauli hiyo imetolewa kama njia ya kujinadi.
“Kama mtu wa upinzani lazima ajionyeshe kama upande wa pili hawafanyi vizuri ili wao wapigiwe kura na hata waliopo madarakani vilevile,” alisema Ndunguru.
Inahusishwa na fitina za uchaguzi
Hata hivyo upo uhusiano wa kile kinachofanywa na watu hao dhidi ya Rais Samia na fitina za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Hilo linathibitishwa na kilichoelezwa Aprili 11, mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba aliyesema miongoni mwa nyakati ambazo ndani ya CCM kunashamiri fitina ni pale Uchaguzi Mkuu unapokaribia huku Rais aliyepo madarakani akipaswa kuendelea na muhula wa pili.
Akizungumza mbele ya wananchi wa Kijiji cha Mahezangulu mkoani Tanga, Makamba alisema katika nyakati hizo watu ndani ya chama hicho hufanyiana fitina.
“Kwenye CCM kipindi kikubwa cha kufitiniana huwa ni hiki, tunapokuwa na Rais anayeendelea ambaye anapaswa kuendelea basi kama vile ada kwenye CCM watu kusema unaona huyu bwana, hataki huyu aendelee, umeona huyu bwana anazamazama ili aonekane huyu hafai, umeona huyu bwana anatega huyu ashindwe,” alisema.
Hata hivyo, mwanasiasa huyo alieleza aghalabu fitina hizo hukoma siku ambayo mgombea huyo anayepaswa kuwania urais kwa muhula wa pili anapokwenda kuchukua fomu.
“Kwa hiyo tuendelee kuombeana hii fitina pia isiwe na mashiko kwenye nchi yetu na chama chetu na bahati nzuri muda utafika kwa sababu mwakani itapangwa tarehe, anayechukua fomu anakuwa huyu mmoja, siku hiyohiyo ile fitina imekufa,” alisema.
Katika hotuba yake hiyo, mwana huyo wa Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuph Makamba aliweka wazi kuwa, pamoja na fitina zote zinazofanyika, lakini wakati ndiyo unaoamua atakayetwaa wadhifa huo.
Alisisitiza katika uchaguzi mkuu wa mwakani, mgombea pekee atakayegombea nafasi hiyo ni Rais Samia, kama ulivyo utaratibu wa siku zote wa chama hicho.
Kikwete
Mbali na Makamba Desemba 8, 2022 katika mkutano mkuu wa 10 wa CCM, Rais Mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete alidokeza kuhusu fitina kuelekea uchaguzi.
Katika kipindi hicho, Kikwete alisema maneno ya uongo huwa mengi, ikiwemo watakaosema fulani anaungwa mkono na mzee huyu, akisisitiza hayo yote ni upuuzi.
"Utasikia kijana gani atagombea, mzee gani atagombea huo ni upuuzi mtupu, sio kama nawazuia lakini simuoni mwana-CCM atakayechukua fomu kukupinga 2025 labda mambo yaharibike sana sasa na wakati huu," alisema.
Alimwambia Rais Samia asibabaishwe na maneno, ambayo hata wakati wake (alipokuwa Rais) yalikuwepo.
"Wapo watakaosema waziri gani kakusanya pesa, hao wote ni waganga njaa, kipindi changu yalikuwepo maneno kama hayo kwa bwana fulani aliyejiita mwanaharakati, lakini ni uongo mtupu,” alisema.
Mkuu huyo wa nchi mstaafu, aliwataka makada wa chama hicho kuacha uongo kwani unawatengenezea viongozi msongo wa mawazo.
"Naombeni tuache uongo, mnawatengenezea viongozi wetu stress (msongo wa mawazo) zisizokuwa na msingi, badala ya kukusanya nguvu zao kujenga Chama na kutimiza majukumu yao ya kikatiba wanaanza kuangaikia upuuzi wenu, this is not fare (hii sio sawa)," alisema Rais Kikwete huku akishangiliwa kwa nguvu na kuongeza. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amesema miongoni mwa nyak | Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amesema miongoni mwa nyakati ambazo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kunashamiri fitina ni pale Uchaguzi Mkuu unapokaribia huku Rais aliyepo madarakani akipaswa kuendelea na muhula wa pili.
Kauli ya Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli mkoani Tanga, inaakisi kile ambacho aghalabu kinashuhudiwa ndani ya chama hicho tawala, unapokaribia Uchaguzi Mkuu hasa unaomuweka Rais aliyepo madarakani katika kipindi cha pili.
Ni utaratibu wa CCM, Rais anayetokana na chama hicho anapomaliza muhula mmoja wa miaka mitano ya uongozi wake, hapaswi kuwekewa pingamizi na mwanachama mwingine, anapowania kipindi cha pili katika uchaguzi unaofuata. Ingawa hilo si sharti la katiba ya chama hicho.
Utaratibu huo huo ndiyo unaotarajiwa kutumika kumuachia Rais Samia Suluhu Hassan awanie kipindi cha pili cha urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kwa mujibu wa Makamba, hapo ndipo fitina ndani ya chama hicho zinaposhamiri.
Hata hivyo, hoja ya Makamba kuhusu fitina inashabihiana na matukio kadhaa katika chaguzi zilizopita ukiwemo mwaka 2010, ambapo aliyekuwa kada wa chama hicho, John Shibuda alitangaza nia ya kuwania urais, katika kipindi ambacho Jakaya Kikwete alikuwa anawania muhula wa pili.
Mbali na hilo, unapoakaribia uchaguzi kama huo, ndani ya chama hicho kumekuwa na minong’ono mbalimbali kuhusu wanaowania kiti cha urais, kumpinga anayepaswa kuendelea.
Hata hivyo, Katibu Mkuu wa CCM, John Nchimbi ingawa hakufafanua kuhusu fitina katika nyakati hizo, lakini alisema ipo wazi juu ya utararibu wa chama hicho katika uchaguzi wa mwaka 2025.
Makamba alitoa kauli hiyo katika moja ya hotuba zake mbele ya wananchi wa Kijiji cha Mahezangulu mkoani Tanga, wakati wa maulidi ya 40 inayofanyika kila mwaka siku ya Idd pili jimboni kwake.
Kwa mujibu wa Makamba, katika nyakati hizo watu ndani ya chama hicho hufanyiana fitina.
“Kwenye CCM kipindi kikubwa cha kufitiniana huwa ni hiki, tunapokuwa na Rais anayeendelea ambaye anapaswa kuendelea basi kama vile ada kwenye CCM watu kusema unaona huyu bwana, hataki huyu aendelee, umeona huyu bwana anazamazama ili aonekane huyu hafai, umeona huyu bwana anatega huyu ashindwe,” alisema.
Hata hivyo, mwakasiasa huyo alieleza aghalabu fitina hizo hukoma siku ambayo mgombea huyo anayepaswa kuwania urais kwa muhula wa pili anapokwenda kuchukua fomu.
“Kwa hiyo tuendelee kuombeana hii fitina pia isiwe na mashiko kwenye nchi yetu na chama chetu na bahati nzuri muda utafika kwa sababu mwakani itapangwa tarehe, anayechukua fomu anakuwa huyu mmoja, siku hiyo hiyo ile fitina imekufa,” alisema.
Katika hotuba yake hiyo, mwana huyo wa Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuph Makamba aliweka wazi kuwa, pamoja na fitina zote zinazofanyika, lakini wakati ndiyo unaoamua atakayetwaa wadhifa huo.
Alisisitiza katika uchaguzi mkuu wa mwakani, mgombea pekee atakayegombea nafasi hiyo ni Rais Samia, kama ulivyo utaratibu wa siku zote wa chama hicho.
Alitumia jukwaa hilo kueleza hatua ya Tanzania kuongozwa na Rais Samia ni baraka, kwa kuwa ni kiongozi mwenye busara na hekima, mambo yanayochagiza maendeleo, amani na utulivu nchini.
Aliwataka wananchi hao, wafanye maombi kwa mkuu huyo wa nchi afanikiwe katika uongozi wake hadi mwaka 2030.
"Tumuombee Rais wetu afya njema na mafanikio katika uongozi wake ili kusitokee rabsha, shari na vurugu zikazokwamisha mipango na malengo yake,” alisema.
Alichosema Nchimbi
Kutokana na kauli hiyo Katibu Mkuu wa CCM, Nchimbi aliliambia Mwananchi kuwa, ni wazi inajulikana kuhusu uchaguzi wa muhula wa pili wa urais wa mgombea wa CCM, ingawa alisisitiza kwa sasa chama hicho kimeelekeza juhudi zake katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
“Jambo liko wazi. Lakini kwa sasa niseme tu tumejikita katika maandalizi ya uchaguzi wa serikali za Mitaa uliopo mbele yetu,” alisema.
Katika kauli yake hiyo, Dk Nchimbi alisema ukifika wakati wa uchaguzi mkuu, atazungumza zaidi akidokeza, “hatuwezi kuzungumza kabla ya kulivuka daraja.” |
Serikali imetangaza rasmi mabadiliko ya jina la Tume ya Taifa la Uchaguzi (NEC) kuwa Tume Huru ya Ta | Serikali imetangaza rasmi mabadiliko ya jina la Tume ya Taifa la Uchaguzi (NEC) kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Mabadiliko hayo yanakuja siku chache baada ya uliokuwa muswada wa sheria ya tume ya taifa ya uchaguzi, kuwa sheria rasmi kutokana na kupitia michakato yote halali.
Muswada wa sheria hiyo na nyingine tatu, iliwasilishwa bungeni mwaka jana, ikilenga kufanyiwa marekebisho ili kuboresha utendaji wa tume na mchakato wa uchaguzi.
Baada ya kukamilika kwa mchakato wa bungeni, kilichokuwa kinasubiriwa ni saini ya Rais Samia Suluhu Hassan ili sheria hiyo iwe rasmi na Machi 29, mwaka huu.
Hata hivyo, kulikuwa na upinzani mkali kutoka kwa wanasiasa wav yama vya upinzani dhidi ya sheria hiyo, wakidai mabadiliko yake hayajakidhi mahitaji yao.
Miongoni mwa yaliyohitajika na upinzani katika mabadiliko hayo ni uchaguzi wa serikali za Mitaa usimamiwe na tume badala ya tawala za mikoa, jambo ambao limebaki kama lilivyokuwa.
Mengine ni kuwepo kwa mgombea binafsi, nalo bado mabadiliko ya sheria hayajagusia hilo, hivyo Tanzania inabaki katika msingi kwamba mtu asiye na chama hatakuwa na haki ya kuwania nafasi ya uongozi wa kisiasa.
Taarifa kuhusu mabadiliko ya jina la NEC, imetolewa leo Jumatano, Aprili 10, 2024 na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi.
Katika taarifa hiyo Matinyi ameweka wazi kuwa, rasmi mabadiliko ya jina la tume hiyo yataanza rasmi Aprili 12, mwaka huu.
Kuanza kutumika kwa jina hilo, amesema kutaambatana na kuanza kutumika kwa sheria hizo mpya zilizotangazwa katika gazeti la Serikali mwishoni mwa Machi, mwaka huu.
“Tunapenda kuvitaarifu vyombo vyote vya habari kwamba, kufuatia tangazo la Serikali Na. 225 la Machi 29, mwaka huu, Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya mwaka 2024, itaanza kutumika rasmi Aprili 12, 2024,” imeeleza taarifa ya Matinyi.
Kwa mujibu wa Matinyi, kuanzia Aprili 12 mwaka huu, jina la tume litabadilika kuwa ‘Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na kwa Kiingereza itaitwa INDEPENDENT NATIONAL ELECTORAL COMMISSION. |
Msisitizo kuhusu Watanzania kujitokeza kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ni moja ya ujumbe uli | Msisitizo kuhusu Watanzania kujitokeza kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ni moja ya ujumbe ulioguswa katika sehemu kubwa ya hotuba za viongozi wa dini ya kiislamu wakati wa ibada ya swala ya Idd El Fitri iliyofanyika maeneo mbalimbali nchini.
Pamoja na ushiriki wa waumini wa dini hiyo katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika mwaka huu, hotuba nyingine ziliweka msisitizo kwenye matendo mema yaliyofanywa ndani ya mwezi wa Ramadhan, yaakisi mema katika uchaguzi unaotarajiwa.
Msingi wa jumbe hizo kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa katika hotuba za viongozi hao wa dini ndani ya ibada hiyo, inatokana na ukweli kwamba, imebaki miezi michache kabla ya uchaguzi huo kufanyika.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao kalenda yake itatangazwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), utafuatiwa na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwakani.
Ibada ya Eid hufanyika kila mwaka ikiwa ni mwanzo wa sherehe ya waumini wa dini ya kiislamu baada ya kuhitimisha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa takriban siku 30.
Ujumbe wa uchaguzi
Ujumbe kuhusu uchaguzi ulianza kutolewa na Sheikh wa msikiti wa Mtoro, Kariakoo jijini Dar es Salaam, Abdallah Mohammed aliyewataka waumini wa dini hiyo kutumia mafunzo ya mwezi Ramadhan kudumisha amani katika uchaguzi wa kuwapata viongozi wa kitaifa.
Kwa mujibu wa Sheikh huyo, chaguzi aghalabu huambatana na mambo mengi na amani ndiyo msingi wa kuvuka kwa usalama na kupatikana kwa kiongozi sahihi.
Aliwataka waumini wa dini hiyo kuhakikisha matendo yao ya mwezi wa Ramadhan yanaakisi mema katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
"Tunakwenda katika uchaguzi (uchaguzi wa Serikali za mitaa) kunakuwa na matatizo mengi ndani yake, ili tuvuke salama msingi wake ni amani kwa hiyo Waislamu wawe watulivu kama walivyokuwa kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhani," amesema.
Katika mkoa wa Mwanza, waumini wa dini hiyo walitakiwa kuacha tabia ya kutoshiriki uchaguzi, huku wakisisitizwa pia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.
Ujumbe huo ulitolewa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Hassan Kabeke wakati wa ibada ya Idd iliyofanyika katika viwanja vya Nyamagana.
Alitumia hotuba yake, kuwasihi waislamu kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
"Nchi yetu inaingia katika uchaguzi, nitumie nafasi hii kuwaasa waumini wenzangu kushiriki katika uchaguzi huo, itakapotangazwa daftari la kujiandikisha nenda kajiandikishe na tunafahamu nchi ina vyama vingi chagua chochote kagombee nafasi yoyote ya uongozi iwe mwenyekiti wa Mtaa, Kijiji, Kata, Diwani, Ubunge au hata Uraisi nenda usibaki kulalamika," alisema.
Katika hotuba yake hiyo, aliwataka waumini hao kuacha tabia ya kuwadharau wanawake wanapopewa mamlaka, akifafanua kufanya hivyo kunakwaza maendeleo.
"Hatuna nafasi ya kumdharau mwanamke hasa akiwa amechaguliwa na Mungu kwa sababu hakuna mtu anayepata mamlaka bila Mungu kumpa kibali na katika nchi yetu kwa sasa ni Rais Samia Suluhu Hassan tumuombee ili alizidi kupata kibali mbele za Mungu," alisema.
Singida nako, Sheikh wa mkoa huo, Issa Nassoro aliwataka waislam kujitokeza kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi wa serikali za Mitaa.
Sheikh huyo alitumia hotuba yake katika ibada ya Idd kufikisha ujumbe huo, akisisitiza kukoma kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi huo.
"Tuepuke kutoa rushwa, kupokea rushwa katika kuyahitaji mambo halali, kama ni haki endelea kusimamia haki yako usitoe shinikizo la kupata haki,” alisema.
Katika Mkoa wa Mbeya, mkuu wa mkoa huo, Juma Homera alitumia jukwaa la ibada hiyo kuwasihi waumini wa dini ya kiislamu kujitokeza katika uchaguzi hasa wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
Kufanya hivyo, alisema kutasaidia kupatikana kwa viongozi bora, huku akikipigia chapuo Chama Cha Mapinduzi (CCM) akisema kinao viongozi wa aina hiyo.
"Tunaposherekea siku kuu ya leo niwakumbushe tuna uchaguzi hivi karibuni wa serikali za mitaa, jitokezeni kwa wingi kuchagua viongozi bora na siyo bora viongozi.
"Ni wazi tunao viongozi imara na bora CCM wakiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, Spika wa Bunge Dk Tulia Akson na wengine tupambane kuwalinda pale uchaguzi Mkuu wa mwakani utakapofika" alisema.
Hata hivyo, Mbunge wa Mbeya Mjini, Dk Tulia aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana katika masuala ya kijamii bila kujali itikadi za vyama, dini na kabila.
"Niwapongeze kwa siku hii, lakini tukumbuke kuendelea kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii kwa kutatua changamoto bila kujali vyama vyetu, dini wala kabila" alisema.
Kuendelezwa mema
Ujumbe mwingine uliobeba uzito wa hotuba za viongozi wa dini hiyo katika ibada ya Idd ni kuendelezwa kwa mema yaliyokuwa yakifanyika katika mwezi wa Ramadhan.
Miongoni mwa waliotoa ujumbe huo ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika ibada hiyo jijini Dodoma, akiwataka Watanzania kuendeleza mema waliyokuwa wakiyatenda wakati wa Mfungo wa Ramadhani na Kwaresima ili kudumisha amani na utulivu nchini.
Akiwa katika msikiti wa Gadaffi mkoani humo, Majaliwa alisema: “Watanzania tunaona kuwa tuna baraka kubwa kupitia mifungo hii miwili Ramadhani na Kwaresima. Kwa hiyo tumejifunza mambo mengi, haya tuliyoyasema yamesisitizwa katika nyumba zote za dini ni wajibu wetu sasa kwenda nayo pamoja.”
Alisema katika mifungo hiyo, viongozi wa dini wamekuwa wakiwaasa waumini kutenda mema na kuachana na maovu.
Rais wa Zanzibar, Hussein Ali Mwinyi naye alilisisitiza hilo, akiwataka waumini waendeleze mema ya mwezi Ramadhan.
Akihutubia katika Baraza la Eid lililofanyika Makao Makuu ya Polisi Zanzibar, Dk Mwinyi alisema ni vema kufanya matendo ya heri katika maisha yote ya mwanadamu.
“Hakika hali tuliyokuwa nayo ya maisha yetu katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ilituongezea uchamungu. Hivyo, namna bora ya kubainisha kufuzu kwetu katika mafunzo tuliyoyapata ni kuyaendeleza mafunzo hayo katika maisha yetu ya kila siku,” alisema.
Wito kama huo ulitolewa na Sheikh wa Mkoa wa Mbeya, Msafiri Njalambaha aliyetaka mema ya mwezi Ramadhan yaendelezwe katika nyakati zote.
"Tuendelee kutenda yaliyo mema kama ambavyo tumefanya kwa kipindi cha siku 30, kurudia maovu ni sawa na kupoteza mwezi mzima wa swaumu na Mungu hatapokea maombi yetu" alisema.
Hotuba hiyo inashabihiana na ile iliyotolewa na Imamu Msaidizi wa Msikiti wa Noor Mirerani mkoani Manyara, Mohamed Shauri aliyewataka waumini wa dini hiyo wasisherehekee sikukuu hiyo kwa kwenda nyumba za kulala wageni na baa.
Akizungumza katika ibada ya Idd mkoani humo, Shauri alisema ni muhimu waumini hao wakasherehekea huku wakizikwepa anasa kama pombe na uzinzi, badala yake waendeleze ibada.
"Leo siyo siku ya kufanya anasa kwa kusherehekea kwenye mapombe, madisko na mikusanyiko mibaya kwani dini yetu haitufundishi hivyo," alisema.
Alisisitiza si vema muislamu kusherehekea sikukuu ya Idd El Fitri akiwa baa anakunywa pombe au nyumba za wageni akifanya uzinifu.
"Hivi sasa baadhi ya baa watanunua viti vipya wakitarajia kupata wateja wao ambao hawakuwa nao kipindi cha mfungo wa Ramadhan hivyo msijitose huko endeleeni kufanya mema na kuachana dhambi," alisema.
Mufti
Msisitizo wa hoja hiyo ulitolewa pia na Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir aliyesema kumalizika kwa mwezi wa Ramadhan kusifungue milango ya maasi kwa waumini wa dini hiyo.
"Siku ya Idd el- Fitri ni siku ya furaha, kuitana kushirikiana na kumuomba Mungu msamaha zaidi, sio siku ya kumuasi Mungu,” alisema baada ya ibada ya Eid iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Mohamed VI, Kinondoni, Dar es Salaam.
Mwingine aliyetoa nasaha za kuendelezwa kwa mema ya Ramadhan ni Sheikh Abdulkareem Nassor alipotubia swala ya Idd katika msikiti wa Jamiatul Zinjibar Mazizini mjini Unguja.
Alisema umoja na mshikamano ulioshuhudiwa kwa waumini wa dini ya kiislamu katika kipindi cha mwezi wa Ramadhani kuna umuhimu wa kuuendeleza.
Kwa mujibu wa Sheikh Nassor, ktika kipindi hicho ameshuhudia wenye uwezo wakiwasaidia wasio nao.
"Saidianeni katika mema na uchamungu na wala msishindane katika mambo mabaya kwani kufanya hivyo ni kumkosea Mungu"alisema.
Aliwataka waumini hao kuunga mkono maendeleo yanayofanywa na viongozi, kadhalika wawaheshimu, akifafanua hilo limeelekezwa hata katika hadithi mbalimbali ndani ya dini ya kiislamu.
Aliyefunga nasaha hizo ni Seikh Ally Musa aliyehutubia katika ibada ya sikukuu hiyo katika viwanja vya Shule ya sekondari ya Forest Hill Manispaa ya Morogoro.
Sheikh Musa alisema ni muhimu kwa waumini kuendeleza sala na toba kila wakati, badala ya kuyaacha mema mara tu Ramadhan inapomalizika.
"Leo ni siku ya huzuni na furaha kwetu, wengi tunasherehekea siku kuu ya Idd El Fitri lakini wakati tunasherehekea tunapata huzuni kwa kuwa waislamu waliowengi watayaacha yale mema yote waliyoyatenda kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,” alisema.
Alieleza katika mwezi huo, waumini walijizuia kufanya matendo mabaya na sasa baadhi hukengeuka baada ya mwezi huo kuisha.
Mvua yakatisha ibada Kigoma
Wakati kwingineko ibada zikiendelea, waumini wa dini hiyo waliopanga kuswali Idd katika viwanja vya Shule ya Msingi Ujiji wameshindwa kutekeleza ibada hiyo, baada ya mvua kubwa kunyesha.
Mvua hiyo ilianza kunyesha muda mchache baada ya swala kuanza na hivyo kulazimu waumini wakatishe ili kujikinga.
Katika eneo hilo, swala ya Idd ilipangwa kuanza saa 3:00 asubuhi lakini kutokana na dalili hiyo ya mvua swala hiyo ilianza saa 2:45 lakini bado kuwahi huko hakukufanikisha ibada kukamilika.
Ujume wa Rais Samia, Mbowe
Kwa upande wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na kuwataka heria ya sikukuu hiyo Watanzania, alitumia kurasa za mitandao yake ya kijamii, kumuomba Mungu abariki uwepo wa amani, haki, umoja na mshikamano nchini.
Katika ujumbe wake huo kupitia mitandao ya kijamii, mkuu huyo wa nchi aliandika ombi kwa Mwenyezi Mungu juu ya kumuongoza katika kusimamia misingi ya kufanya mema na moyo wa shukurani.
“Mwenyezi Mungu atuonaye tunaposimama na mageuko yetu kati ya wanaosujudu, Mwenye kusikia na kupokea dua zetu; aendelee kutubariki na kudumisha Taifa letu katika haki, umoja, amani na mshikamano; katika misingi ya kufanya yaliyo mema, kujali na kutumikia wengine kwa upendo na weledi, na mioyo iliyojaa shukrani na ibada kwake. Idd Mubarak,” aliandika.
Jukwaa la mitandao ya kijamii, lilitumiwa pia na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyeandika ujumbe wa kuwatakia mema waumini wa dini ya kiislamu, kadhalika amani, furaha na baraka.
“Tunaposherehekea mwisho wa Ramadhani, tukumbuke masomo ya subira, huruma, haki, na shukrani ambayo mwezi huu mtukufu umetufundisha. Tuendeleze roho ya umoja, haki na ukarimu tunapoadhimisha siku hii maalum,” unasomeka ujumbe huo.
Kadhalika, mwanasiasa huyo alisisitiza kuenezwa kwa upendo, wema, haki na uelewano katika jamii, huku akitaka matendo ya waumini hao yaakisi kiini cha kweli cha Uislamu. |
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema haonei aibu urafiki wake binaf | Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema haonei aibu urafiki wake binafsi na sehemu kubwa ya viongozi wa vyama vya upinzani.
Msingi wa kauli yake hiyo ni kile alichofafanua kuwa, huwezi kujivunia utanzania kama huna mapenzi na Watanzania wenzako, hivyo itikadi za vyama haziwezi kukwaza urafiki wake na watu.
Mtendaji Mkuu huyo wa CCM alitoa kauli hiyo jana wakati akihutubia Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere lililoandaliwa na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA).
Aliijenga hoja hiyo kwa kurejea kile alichokiita matendo ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambaye katika enzi za uhai wake aliwapenda Watanzania wote bila kuwabagua.
Kuhusu urafiki na viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani, alisema haoni haya juu ya hilo na kwamba mara nyingi amekuwa akiwasiliana nao kila wanapoonekana wamezungumza hasa vibaya majukwaani.
"Viongozi wengi wa upinzani ni rafiki zangu binafsi na mara nyingi wakishaongea kwenye mikutano yao kama wameongea kitu kibaya huwa nawatumia ujumbe kuwaeleza kwamba ulichozungumza leo kama Watanzania wamekusikia basi wamehisi umevuta bangi.
"Unakuta ananipigia tunazungumza, tunacheka na mwisho wa siku tunamaliza mazungumzo, ndivyo ambavyo Watanzania tunapaswa tuishi," alisema.
Alisisitiza misingi ya utanzania ni kuwapenda Watanzania wenzako bila kufikiria ubaguzi wa kiitikadi, rangi, wala kabila.
Katika hotuba yake hiyo, Dk Nchimbi alisema kwenye uongozi wa sasa ni vema kumteuwa kiongozi kulingana na kaliba yake.
Alieleza wapo baadhi ya watu wenye uwezo mkubwa katika kuhamasisha maendeleo, lakini wanapopitiwa na fedha karibu lazima waibe.
"Sasa mtu kama huyu inabidi umpeleke katika eneo ambalo atafanya hiyo kazi ya kuhamasisha maendeleo ili usiukose ule ufanisi wake lakini asiwe karibu na fedha, kama ni mzuri kwenye kusimamia fedha mpeleke huko," alisema.
Hoja ya ukaribu wa Dk Nchimbi na wanasiasa wa upinzani, iliungwa mkono na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazani Tanzania (TBC), Dk Ayubu Riba aliyesema mwenendo huo ndiyo nyenzo ya uongozi bora.
Alisema ili kuwa kiongozi bora ni vema utoe nafasi ya kusikiliza wengine wakiwemo wanaokupinga.
Akemea wizi
Alitumia jukwaa hilo, kueleza uwepo wa sehemu kubwa ya Watanzania ambao aghalabu wanapoongelea nafasi ya uongozi akili zinawapeleka kwenye kupiga dili.
"Robo tatu ya watu wakiongelea nafasi ya uongozi, akili yao inawapeleka kwenye kupiga dili," alisema.
Alisema akili hizo ni matokeo ya kwenda kinyume na misingi ya Baba wa Taifa juu ya kupenda kazi.
"Mara nyingi asiyependa kazi hupendelea kupata kwa urahisi, ili apate kwa urahisi ataiba na mwizi mara zote yupo tayari kuuwa," alisema.
Alisema msingi wa mambo yote ni kutoandaliwa kwa viongozi kama ilivyokuwa ikifanyika zamani.
Alieleza Mwalimu Nyerere alitumia nguvu kubwa kuandaa viongozi na hata wakati anakaribia kung'atuka alihangaika kumtafuta mrithi.
"Ndiyo sababu hata alimtafuta Edward Sokoine akamuona anafaa katika wadhifa wa Waziri Mkuu, lakini alimuona hana exposure na ikabidi ampeleke nje ya nchi kusoma," alisema.
Alisisitiza umuhimu wa kuendelezwa kwa utaratibu wa kuandaliwa kwa viongozi na kwamba usiishie katika Chuo cha MNMA pekee, bali viwepo na vingine vitakavyoifanya kazi hiyo.
Hata hivyo, alisema ni muhimu kuwepo vyuo vinavyofundisha wananchi kutoka katika vyama vyote na kuwe na namna ambayo kila chama kiwe na mchango.
"Si wajibu wa CCM peke yake, lazima Chama kinachotawala na vya upinzani vikae chini kukubaliana muundo wa Taasisi ya Elimu kwa wanasiasa wake," alisema.
Alisema kila Mtanzania anapaswa kujua kuwa anao wajibu kwa taifa lake.
Akichangia mada kuhusu amani, umoja, na uwajibikaji katika ujenzi wa taifa, Mkufunzi wa Chuo cha Uongozi cha Julius Nyerere, Kanali Joseph Simbakalia alisema chama cha TANU ndicho kilichojenga misingi yote ya nchi.
Hata hivyo, alisema ili kuwepo na amani kunahitajika umoja kwanza.
"Ni jambo la fahari ulitengenezwa umoja na baadaye ukaja umoja wa taifa unaotokana na Tanganyika na Zanzibar na kuunda Tanzania," alisema
Alitoa taarifa ya Chuo, Mkuu wa chuo hicho, Profesa Shadrack Mwakalila alisema tangu mwaka 1961 ambapo chuo hicho kilianzishwa viongozi 2,000 wamepata mafunzo ya uongozi.
Alisema chuo hicho kilimilikiwa na CCM hadi mwaka 1991 kilipokabidhiwa kwa Serikali na mwaka 2005 kikabadilishwa jina kutoka Chuo cha Kivukoni hadi Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
"Kwa sasa chuo hiki kina matawi matatu, ikiwemo Kivukoni, Karume, Bugugu Unguja na Pemba katika Wilaya ya Chakechake," alisema.
Alisema kwa sasa chuo hicho kimeongeza masomo ya uongozi, maadili na uzalendo katika mitalaa yote ili kila mwanafunzi anayehitimu chuoni hapo awe na ujuzi kuhusu masuala hayo.
Akimzungumzia Mwalimu Nyerere, Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, Stephen Wassira alisema hadi sasa iwapo angekuwa hai kiongozi huyo angekuwa na umri wa miaka 102.
"Mwalimu Nyerere alitoa mchango mkubwa wa ukombozi wa Kusini mwa Afrika na ilitokana na imani kwamba uhuru wa Tanzania hautakuwa na maana iwapo nchi nyingine hazina huru," alisema. |
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson ametoa wito kwa taasisi mbalimbali zikiwemo za kifedha kujenga utara | Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson ametoa wito kwa taasisi mbalimbali zikiwemo za kifedha kujenga utaratibu wa kurudisha fadhila kwa jamii, akisema kufanya hivyo ni ibada yenye tija kwa taasisi husika.
Dk Tulia ametoa kauli hiyo jijini Dodoma, alipozungumza baada ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya NMB kwa Viongozi wa Serikali, Wabunge na watoto yatima wanaolelewa katika vituo vya Zam Zam na Darul Maarifu.
Katika maelezo yake hayo, Spika huyo ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), amerejea maandiko ya kitabu cha Quran yanayoeleza umuhimu wa kutenda wema kwa makundi hayo.
“Katika Qur-an Tukufu Surah ya 99 (Az Zalzalah), aya ya saba hadi ya nane – inayosema, basi yule mwenye kutenda wema mdogo mfano wa mdudu chungu, atalipwa na mwenye kutenda uovu au ubaya mdogo mfano wa sisimizi, atalipwa,” alisema.
Katika wito wake kwa taasisi hizo, Dk Tulia aliitolea mfano benki ya NMB kama kielelezo cha kurudisha kwa jamii, akirejea utaratibu wa taasisi hiyo ya fedha, kufuturisha watu katika Mikoa mbalimbali.
“Tunaithamini sadaka hii, tunawapongeza NMB kwa kazi nzuri, na hii ni kwa niaba ya wote waliofuturu hapa na ambao hawawezi kupata fursa ya kuongea, naomba mfahamu tu kuwa tunaheshimu sana sadaka hii mliyoitoa leo hapa na kule kote mlikofuturisha,” amesema.
Kwa mujibu wa Spika huyo, hatua ya kufuturisha makundi hayo ni sawa na kuisaidia jamii ambayo kimsingi ndiyo wapigakura.
“Tunawapongeza kwa sababu mmeenda kuwafuturisha wapiga kura wetu huko,” ameeleza Dk Tulia.
Kwa hicho kinachoendelea kufanywa na benki hiyo, amesema kitaipa matokeo zaidi taasisi hiyo na kwamba katika miaka ijayo shughuli kama hicho zitakuwa nyingi zaidi.
Awali, akizungumza katika shughuli hiyo, Ofisa Mkuu wa Fedha wa NMB, Juma Kimori amesema ni muda mrefu tangu taasisi hiyo ilipoanza ufuturishaji wa wateja, waumini na wadau wake.
Kilichoisukuma taasisi hiyo kulitekeleza hilo ni kile alichoeleza kuwa, imebaini uwepo wa watu wengi wenye uhitaji.
“Kila mwaka huwa tunafanya hafla hizi, lengo ni kudumisha ukaribu na kustawisha mahusiano mema na jamii inayotuunga mkono,” amesema.
Ameeleza futari kwa makundi ya watoto hao, inawahamasisha kufanya matendo mema mbele ya jamii, pindi watakapokuwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Dk Edwin Mhede amesema mbali na kukutana kwa ajili ya Iftari, shughuli hiyo pia inawawezesha kuzungumza mambo mbalimbali na kukumbushana mema.
“Ukiachana na ukweli kwamba hii ni ibada, lakini kwanini tunakutana? Kitabu Kitukufu cha Qur ani kinatuasa na kutuhimiza umuhimu wa kukutana na kukumbushana, kwani inaaminika kwamba katika kukumbushana, ndiko tunakoweza kujengana vizuri kabisa,” amefafanua Dk. Mhede.
Mwisho.
Jumla ya wafanyabiashara 18 walioathiriwa na maporomoko ya tope wilayani Hanang mkoani Manyara, wanatarajiwa kulipwa Sh270 milioni, ikiwa ni fidia ya mikopo kutoka Benki ya NMB.
Kulingana na NMB, wafanyabiashara hao walikopa katika benki hiyo mikopo yenye kinga ya bima kutoka kampuni ya Reliance Insurance.
Hatua hiyo ya NMB inakuja, wakati Serikali pia ilishaonyesha nia ya kuwakopesha wafanyabiashara hao ili warudishe mitaji yao, huku waliopoteza makazi wakitarajiwa kujengewa nyumba za kati ya Sh25 milioni hadi Sh30 milioni.
“Wale watu siku nimeonana nao kambini, walisema tumebaki sisi tu, mwingine alikuwa na mume ameachiwa watoto, lakini walinambia mashamba na vijumba vyetu vyote vimeondoka nikatoa ahadi kwao. Niliwaambia hakuna atakayebaki na shida,” alisema Rais Samia alipozungumza katika tukio hilo, Desemba mwaka huu.
Taarifa ya kulipwa kwa wafanyabiashara hao, ilitolewa jana na Mkuu wa Idara ya Bima ya NMB, Martine Massawe alisema nafuu ya hasara waliyopata wafanyabiashara hao imetokana na kuwa na kinga ya bima.
Alisisitiza umuhimu wa wafanyabiashara kuwa na bima, akisema ndiyo huduma inayosaidia kuzikabili hatari za kibiashara yanapotokea majanga.
"Wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo hukabiliwa na changamoto nyingi na matukio yasiyotarajiwa hivyo kutokuwa na uhakika wa usalama na uendelevu wa shughuli zao.
“Kwa mantiki hiyo, bima ni kitu muhimu kwa ajili ya kutoa ahueni kwa wahanga wa athari zinazohatarisha maisha na mafanikio yao,” alisema Massawe.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja alisema utafitiwa awali uliofanyika kubainisha ukubwa wa janga sit u ulibaini kuathirika kwa mamia ya wajasiriamali, bali pia uligundua wengi hawakuwa na bima na hawafahamu faida zake.
“Kimsingi kiwango cha elimu kuhusu huduma za bima katika Wilaya yetu bado kiko chini sana na hakuna mtu aliyewahi kufikiria kuwa Wilaya yetu ingekumbwa na janga kama hili.
“Kama tunataka kusonga mbele tukiwa na uhakika wa usalama wa maisha na mali zetu, wote sasa tunatakiwa kuanzisha utamaduni wa kuwa na kinga ya bima na kuzitumia bidhaa zake mbalimbali,” alisema.
Mmoja wa wanufaika wa fidia hiyo, Hapiness Mlay aliyelipwa Sh28.5 milioni, aliwasihi wafanyabiashara wenzake kuhakikisha wanakuwa na huduma hiyo ili kujikinga wanapopata athari.
Akizungumza katika hafla hiyo, Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dk Baghayo Saqware alizitaka kampuni za bima kulipa kipaumbele suala la unafuu wa gharama za huduma.
“Hivi sasa, watoa huduma mbalimbali wa bima wamebuni bidhaa mbalimbali za bima ili kuwavutia watumiaji wengi. Natumia fursa hii kuwakumbusha wananchi wote kuchangamkia fursa hii kikamilifu ili kupunguza athari za majanga,” alisema. |
Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango anatarajia kuiwakilisha Tanzania katika mkutano wa Jukwaa la Uchumi | Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango anatarajia kuiwakilisha Tanzania katika mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) utakaofanyika kesho hadi Januari 19, mwaka huu.
Katika mkutano huo, utakaofanyika nchini Uswisi, Dk Mpango atashiriki akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, aliyebaki nchini kwa majukumu mengine.
Taarifa ya safari ya Dk Mpango imetolewa leo, Jumapili Januari 14, 2024 na kutiwa saini na Msaidizi wake wa Habari, Franco Singaile.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Dk Mpango anatarajiwa kuhudhuria mikutano mbalimbali katika jukwaa hilo, ikiwemo inayohusu uchumi, uwekezaji na utawala bora.
Mikutano mingine atakayohudhuria katika jukwaa hilo ni kilimo, usalama wa chakula na mabadiliko ya tabianchi. Kadhalika kiongozi huyo atafanya mazungumzo na viongozi wa mataifa na mashirika mbalimbali ya kimataifa.
Wengine atakaofanya nao mazungumzo ni watendaji wakuu wa mashirika ya kimataifa, wakuu wa taasisi na kampuni duniani na wafanyabiashara.
Kuhusu WEF
Jukwaa la uchumi duniani ni shirika lisilo la kiserikali linaloshughulika na ushirikiano kati ya sekta binafsi na ya umma na karibu kila mwishoni mwa Januari huandaa mkutano wa jukwaa la uchumi duniani.
Mikutano hiyo inawakutanisha wakuu wa mataifa mbalimbali duniani, wanauchumi na wafanyabiashara.
Kauli mbiu ya jukwaa hilo mwaka huu ni ‘Kujenga upya uaminifu’ ikilenga kurejesha imani kwa wakati ujao, ndani ya jamii na miongoni mwa mataifa.
Tanzania inakwenda kushiriki jukwaa hilo, ikiwa na rekodi ya kuimarika, kwa mujibu wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) Oktoba mwaka jana, pato la taifa limekuwa na kufikia Sh200 trilioni mwaka 2023.
Ongezeko hilo ni kutoka Sh163.5 trilioni mwaka 2021 wakati Rais Samia Suluhu Hassan anaingia madarakani.
Hata hivyo, takwimu hizo zinaonyesha pato hilo linaweza kuongezeka na kufikia Sh276 trilioni mwaka 2028.
Kuhusu mkutano wa mabadiliko ya tabianchi katika jukwaa hilo unafanyika huku tayari Tanzania ikiwa na misimamo minne iliyoiweka wazi katika mkutano wa jukwaa la mabadiliko ya tabianchi nchini Misri.
Misimamo hiyo ni kupatikana kwa fedha za ufadhili kwa kuzingatia athari za mabadiliko ya tabianchi, kuanzishwa kwa mfuko wa pamoja wa majanga na maafa kufidia waathirika wa mabadiliko ya tabianchi, matumizi ya nishati safi na jumuishi na mjadala wa jinsia unaompa mwanamke kipaumbele.
Katika eneo la uwekezaji, Kituo cha Uwekezaji (TIC) kimewahi kuweka wazi kuwa, Tanzania imesajili miradi 504 yenye thamani ya Sh10 trilioni kati ya Januari hadi Desemba mwaka jana.
Idadi hiyo ni ongezeko la 100 ikilinganishwa na miradi 132 iliyosajiliwa mwaka 2022. |
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameeleza alivyoruka kiunzi cha shinikizo la kusitisha vibali vya kua | Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameeleza alivyoruka kiunzi cha shinikizo la kusitisha vibali vya kuagiza mchele kutoka Tanzania, huku akitaja sababu nne zilizochagiza asipige marufuku hiyo.
Hatua ya Museveni kutakiwa kupiga marufuku uingizaji wa mchele wa Tanzania katika nchi yake, lilitokana na kile alichoarifiwa kuwa, bidhaa hiyo imeuwa watu kadhaa wa Uganda.
Hata hivyo, mkuu huyo wa nchi ya Uganda, amesema alikataa kupiga marufuku hiyo kwa kuwa yeye si kipofu na kwamba angelifanya hivyo Tanzania na Uganda zingeingia katika kile alichokiita mchezo wa kitoto yaani kulipiana kisasi.
Museveni alitoa kauli hiyo visiwani Zanzibar jana, alipopewa nafasi kutoa salamu za Uganda katika sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika Uwanja wa New Amaan.
“Nyuma kule Uganda waliniambia kwamba mpunga wa Tanzania umetuuwa huku Uganda walikuwa wanataka nipige marufuku mchele wa Tanzania, nikasema siwezi kufanya hivyo, mimi sio kipofu,” alisema.
Iwapo angetekeleza hatua ya kupiga marufuku mchele huo, Museveni alisema angelifanya kile alichokiita dhambi nne.
Alizifafanua dhambi hizo ni kuingia katika mchezo wa kitoto wa kulipiana kisasi kati yake na Tanzania kwa kila nchi kuamua kupiga marufuku uingizaji wa bidhaa za mwenzake.
“Nikifanya hivyo Serikali ya Tanzania nayo italipiza kisasi wanapiga marufuku hiki, mimi napiga marufuku kile, mchezo wa watoto siwezi kufanya namna hiyo,” alisema.
Dhambi nyingine alisema ni kulazimisha Waganda wanunue mchele wa bei ya juu ili kuwatetea wavivu wasiolima kuleta ushindani wa uzalishaji.
Lakini, alieleza kufanya hivyo kungesababisha vikwazo kwa Tanzania ambayo imefikia hatua nzuri ya kilimo cha zao hilo, badala ya kuihamasisha.
“Badala ya kumecourage (kumhamasisha) nampiga kwenye kichwa, hii ni mbaya sana,” alisema.
Kwa mujibu wa Museveni, kufanya hivyo kungesababisha baadhi ya wakulima wa mchele nchini Uganda kuendelea kubweteka kwa kuwa hawatapata shinikizo kutoka kwa mshindani.
Kuhusu mapinduzi, Museveni alisema Serikali ya Hayati Abeid Amani Karume (Rais wa Kwanza wa Zanzibar) ilikuwa na fikra iliyofanana na Uganda, ya kuungana na Tanganyika.
Hata hivyo, alieleza mafanikio ya muungano huo ni matokeo ya juhudi kubwa za wanamajumui wa Afrika.
“Sisi tunakubali na tunaamini kwamba Afrika haiwezi kuendelea bila kuungana. Tumekuwa na mvutano kati ya watu wa aina mbili yaani wanamapinduzi na wale wengine,” alisema.
Alieleza kushangazwa na wanaopinga muungano akisema ama vipofu au wanyonyaji.
“Au ni vipofu au ni wanyonyaji kwa sababu mimi ni mzalishaji mali niko na shida ya soko, huwezi kunambia mambo ya kujitenga tenga kwa sababu nifanye mambo yangu,” alisema.
Rais Mwinyi
Katika hotuba yake katika sherehe hizo, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi alisema Mapinduzi ya miaka 60 yamefikiwa kwa mafanikio, huku akiwapongeza wananchi kwa kudumisha amani.
"Niwapongeze na kuwashikuru viongozi waliotuunga mkono. Tumeadhimisha miaka 60 kwa mafanikio makubwa tunaomba Mungu atusaidie," alisema.
Awali akizungumza kabla ya Dk Mwinyi, Rais Samia Suluhu Hassan alisema miaka 60 ya mapinduzi hayo ndio mwanzo wa safari, huku akiahidi kutengeneza mazingira yatakayorahisisha uzuri wa safari hiyo zaidi.
Hata hivyo, mkuu huyo wa nchi alichapisha ujumbe wa sherehe hizo katika kurasa za mitandao yake ya kijamii akiandika, miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar yamefanyika mageuzi makubwa ya kimaendeleo ikiwemo uboreshaji wa sekta ya afya.
“Sote ni mashahidi wa hatua hizi. Shuhuda mojawapo ni ufunguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi - Lumumba, Zanzibar. Mwaka 1976 nilikuwa mwanafunzi katika Shule ya Lumumba Zanzibar.
“Wakati huo, eneo ilipojengwa hospitali hii mpya ya kisasa palikuwa na zahanati ndogo kabisa iliyoitwa Miwanzini. Kutoka zahanati ile ndogo hadi hapa tulipo leo ni hatua kubwa na ya kujivunia.
Kupitia ujumbe huo, alisema maendeleo ni hatua, jasho na damu na suala endelevu hivyo kuwataka Wazanzibari kuendelea kuwashukuru, kuwapongeza, na kuwaombea dua waasisi wetu ambao waliweka misingi ya kufika hatua hiyo.
“Jukumu sasa kwa kila mmoja wetu ni kutambua tulipotoka, malengo yetu kama taifa na kuendelea kufanya kazi kila mmoja kwa nafasi yake ili kupiga hatua kubwa zaidi huku tukibaki kuwa wamoja, wenye amani na utulivu,” alisema.
Kagame
Kwa upande wa Rais wa Rwanda, Paul Kagame aliwapongeza Wazanzibari kuendeleza malengo na matarajio ya waasisi.
"Muungano huu unaleta ushahidi kwamba Afrika tupo pamoja katika kushughulikia matatizo yetu wenyewe, hakuna kisichowezekana tunapotembea pamoja.
“Hongereni sana na tumedumu sana katika Mapinduzi kwahiyo tunaweza kuungana kama ndgu kama taifa," alisema Kagame
Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua alisema mataifa hayo yanaendelea kushirikiana katika kuleta mendeleo ya nchi hizo za Afrika Mashariki
Waziri Mkuu wa Burundi, Gervais Ndirakobuca alisema taifa hilo halitasahau jinsi Tanzania ilivyowasaidia walipopata matatizo na kuomba udugu huo uendele kudumishwa.
Makamu wa Pili wa Rais, Hemed Suleiman Abdulla alisema zilitumika siku 22 tangu Desemba 20, mwaka jana za kufungua miradi na kuweka mawe ya msingi kabla ya kufikia kilele chake jana.
"Tutaendelea kuyalinda, kuyaenzi na kuyadumisha Mapinduzi haya maana yametuunganisha kutoka katika manyanyaso ya mkoloni na leo yametuletea Maendeleo makubwa," alisema Hemed
Hemed alisema Serikali zote zitaendelea kuwaunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan na Dk Mwinyi.
Ilivyokuwa
Wakati leo ikiwa ni maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi, viongozi mbalimbali wa kitaifa na wananchi wameanza kuwasili katika uwaja wa New Aman Complex zinapofanyika sherehe hizo.
Milango ya kuingia uwanjani ilifunguliwa kuanzia saa 4:00 asubuhi na wananchi walipata fursa kuingia huku wageni waalikwa walianza kuingia saa 7:00 mchana wakifuatia viongozi wakuu wastaafu na wasasa.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan, Ma Rais wa Uganda na Rwanda, Yoweri Museven na Paul Kagame. Burundi iliwakilishwa na Waziri Mkuu wa Nchi hiyo...huku Kenya iliwakilishwa na Makamu wa Rais wa Nchi hiyo...
Rais Mwinyi aliingia uwanjani hapo saa 10:10 jioni akiwa katika gari la wazi, akizunguka uwanja na kuwapungia viongozi na wananchi waliojitokeza kwa wingi katika sherehe hizo.
Baada ya kushuka kwenye gari, alipigiwa mizinga 21, kuimbwa wimbo wa Taifa wa Zanzibar na wimbo maalumu wa mashujaa na kukagua gwaride kabla ya kupanda jukwaani kuketi.
Baada ya kupanda jukwaani kiongozi huyo wa taifa, alipokea maandamano ya vikundi mbalimbali vya wananchi, vyuo vya elimu na taasisi za serikali vikiwa na mabango yaliyokuwa yameandikwa ujumbe tofauti kuhusu mapinduzi.
Gwaride la kijeshi lilipita mbele yake kwa mwendo wa pole na kasi.
Maonyesho ya zana na silaha zinazotumiwa na majeshi ilikuwa kivutio kikubwa kwa wananchi waliohudhuria sherehe hizo
Maonyesho hayo ilikuwa ni pamoja na helkopita mbili zilivyoonyesha jinsi ya kuokoa askari aliyetekwa na kufanikiwa kumuokoa.
Mbali na helkopita, pia yalipita mbele ya Rais magari ya silaha kubwa za kivita.
Katika sherehe hizo, waliozaliwa Januari 12, 1964 ambao walitimiza miaka 60 Jana, walirusha maputo, njiwa uwanjani hapo ikiambatana na wimbo maalumu wa miaka 60 Mapinduzi.
Vikundi maalumu vya kijeshi vilionyesha kazi zao wanamaji, nchi kavu, mabegi mazito
Viongozi wengine wa kitaifa waliohudhuria sherehe hizo ni Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dk Doto Biteko, Spika Tulia Ackson na Zubeir Maulid na Majaji wakuu, Profesa Ibrahim Juma na Khamis Ramadhan Abdallah.
Wengine ni Makamu wa Kwanza na Pili wa Rais, Othman Masoud.
Kwa upande wa viongozi wastaafu alihudhuria Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, Mawaziri wakuu Mizengo Pinda na Fredrick Sumaye. |
Licha ya bei ya sukari kufikia Sh5,000 kwa kilo katika baadhi ya maeneo nchini, Serikali imesema mwe | Licha ya bei ya sukari kufikia Sh5,000 kwa kilo katika baadhi ya maeneo nchini, Serikali imesema mwezi mmoja baadaye bidhaa hiyo inatarajiwa kurejea katika bei ya kawaida.
Kurejea kwa bei hiyo kwa mujibu wa Serikali, kutatokana na hatua iliyochukuliwa na kutoa vibali kwa wazalishaji kuagiza tani 50,000 za sukari, lakini viwanda kuanza kuzalisha.
Hayo yanakuja wakati bei ya sukari katika baadhi ya maeneo imefikia Sh5,000 kwa kilo, huku kwingineko ikiwa kati ya Sh4,000 na Sh4,500, kutoka Sh3,000 iliyokuwepo kwa muda mrefu.
Bei ya bidhaa hiyo imeshuhudiwa ikiongezeka zaidi katika Mkoa wa Arusha ambapo baadhi ya maeneo jijini humo, kilo moja inauzwa Sh5,000 kwa kilo.
Hali kama hiyo, inayakabili baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mtwara, ambapo bei ya sukari imeripotiwa kuongezeka kutoka Sh3,000 hadi Sh5,000 kwa kilo.
Mikoa mingine kama baadhi ya maeneo ya Manyara, kilo moja ya sukari inauzwa Sh4,500 kutoka Sh3,000 ya awali.
Dar es Salaam nako, bei ya bidhaa hiyo kwa kilo iliyoonekana kusimamia Sh3,000 kwa sasa katika baadhi ya maeneo imefika Sh4,000 kwa mujibu wa wananchi.
Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli alisema wazalishaji waliopewa vibali Januari mwaka huu kwa ajili ya kuagiza tani 50,000 za sukari nje ya nchi tayari wameshaagiza.
Kwa sababu uagizaji ni mchakato, alisema inaweza kuchukua takriban mwezi mmoja hadi bidhaa hiyo itakapofika nchini na kuanza kusambazwa.
“Unapoagiza kuna michakato, baada ya kuagiza kuna usafirishaji hadi ifike nchini ni jambo linalochukua takriban mwezi mmoja, kwa hiyo baada ya kipindi hicho ndipo bidhaa hiyo inaweza ikafika,” alisema.
Kwa mujibu wa Mweli, ukomo wa vibali hivyo vilivyotolewa ni mwisho wa mwaka huu wa fedha (Juni 30), hivyo kwa kipindi kilichopo bidhaa hiyo itaendelea kuletwa.
Mbali na tani hizo zilizoagizwa, alisema viwanda vya ndani vimeanza uzalishaji baada ya mvua kupungua na iwapo hali itaendelea kwa wiki mbili, sukari itakuwa nyingi nchini.
“Kama hali ya kupungua kwa mvua itaendelea kwa wiki mbili, tatizo litakwisha kabisa kwa kuwa hivi sasa viwanda vimeanza uzalishaji,” alisema Mweli.
Kuhusu usambazaji wa sukari hiyo iliyoagizwa, Katibu Mkuu huyo alifafanua walioagiza ndiyo watakaosambaza katika maeneo wanayosambazia wakati wote.
“Kila mzalishaji ana eneo lake la kusambaza kwa hiyo hata hii waliyoagiza watasambaza katika maeneo ambayo huwa wanasambaza wanayozalisha.
“Kwa kuwa wazalishaji wapo katika maeneo mbalimbali kila atakayesambaza katika eneo lake atasaidia kupunguza changamoto katika eneo husika,” alisema.
Akizungumzia sababu za kuongezeka kwa bei ya bidhaa hiyo, Mkurugenzi wa Mkulazi Holding Company Limited inayozalisha sukari, Selestine Some alisema gharama za uzalishaji ndiyo mzizi wa tatizo.
Alieleza katika kipindi cha mvua wazalishaji wanakabiliwa na gharama kubwa za uzalishaji wa sukari, ukilinganisha na vipindi vya jua.
Mathalan, alisema katika kipindi cha jua tani 10 za miwa zinaweza kuzalisha tani moja ya sukari, lakini nyakati za mvua utahitaji miwa zaidi kupata tani moja ya sukari.
“Kwa hiyo hapo unaongeza gharama ya uzalishaji hii ndiyo sababu watu wanaona bei ya sukari inapanda kipindi kama hiki,” alisema.
Gharama nyingine za uzalishaji kwa mujibu wa Some, hutokea wakati wa mavuno hadi kufikisha miwa kiwandani.
Alifafanua wakati wa jua kuna kifaa hutumika kukata muwa na kupakia kwenye trela kwa ajili ya kusafirishwa hadi kiwandani, lakini kipindi hiki inalazimu uajiri watu wakakate, wengine wabebe hadi barabarani kisha ndiyo isafirishwe kwenda kiwandani.
Aliitaja sababu nyingine ya kupata kwa bei hiyo, ni kuongezeka kwa mahitaji ya bidhaa husika, huku uzalishaji ukipungua viwandani.
“Panapokuwa na mahitaji makubwa mara nyingi bidhaa inapanda bei huu ni utaratibu wa kawaida kwa kila bidhaa na ndicho kinachotokea hata kwenye sukari,” alisema Some. |
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika ametaka kufutwa kwa miswada | Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika ametaka kufutwa kwa miswada ya sheria za uchaguzi inayotolewa maoni sasa, badala yake upelekwe muswada wa marekebisho ya Katiba.
Miswada aliyopendekeza ifutwe ni ule wa sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na muswada wa sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Mnyika aliliibua pendekezo hilo alipopewa nafasi ya kutoa maoni kuhusu miswada pendekezwa, jambo lililosababisha Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Joseph Mhagama amkatishe.
Sababu za kumkatisha ni kilichoelezwa na Dk Mhagama, kamati hiyo haina mamlaka ya kubadilisha katiba.
“Mheshimiwa John naomba uende kwenye vifungu vya sheria, unajua majukumu ya kamati yetu kwa sababu na wewe ulishawahi kuwa mbunge na kama hauko tayari naomba tutakupa nafasi siku nyingine utakapokuwa tayari kutoa maoni," alisema Dk Mhagama.
Hii si mara ya kwanza kwa Chadema kutaka marekebisho ya Katiba na msingi wa mapendekezo yao ni kuweka mazingira mazuri ya sheria mama kabla ya kuziendea sheria nyingine.
Kabla ya Chadema, wadau wengine wametoa mapendekezo yao wakitaka marekebisho mbalimbali katika miswada hiyo ikiwemo uchaguzi hasa wa Serikali za Mitaa usisimamiwe na Wakurugenzi wa Halmashauri.
Hayo yalitokea jijini Dodoma jana wakati Mnyika alipopewa nafasi ya kutoa maoni kuhusu miswada hiyo mbalimbali ya sheria zinazohusu uchaguzi.
Baada ya kukatishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Mnyika aliachana na hoja hiyo na kuibuka na suala la Wakurugenzi wa Halmashauri kutosimamia uchaguzi.
Katika hoja yake hiyo, Mnyika alitaka watumishi hao wa umma wasipewe nafasi hiyo kwa kuwa si waadilifu.
"Wakurugenzi wengi ndiyo hao ambao kwenye ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wanafanya ubadhirifu wa fedha za umma halafu mnataka wasimamie uchaguzi na watende haki?" alihoji Mnyika.
Aliitaka Tume ya Uchaguzi ya Taifa kuajiri watumishi watakaokuwa wasimamizi wa uchaguzi na si Wakurugenzi wanaoteuliwa na Rais ambaye naye ni mgombea.
Hata hivyo, alipendekeza watumishi hao watakaoteuliwa wanapaswa wawepo wa kudumu kwa ngazi ya halmashauri, huku wengine wakiwa wa mikataba.
Pendekezo lingine, alisema ni uwepo wa kifungu kinachotoa kigezo cha ushindi wa kura za Rais ziwe zaidi ya asilimia 50 na kuwe na mwanya wa matokeo yake kupingwa mahakamani.
“Kwa upande wa nchi za Afrika Mashariki ni Tanzania pekee ambayo matokeo ya Urais hayapingwi,” alisema.
Katika muswada wa sheria ya vyama vya siasa, alipendekeza marekebisho katika kifungu kinachokataza vyama vya siasa kuingiza vifaa vya uchaguzi kutoka nje siku 90 kabla ya uchaguzi mkuu.
“Kama chama kinataka kukodi helikopta kwa ajili ya kampeni ni lazima wazikodi kabla ya siku hizo ambayo ni gharama kubwa,” alisema.
Mbali na Mnyika mwingine aliyetoa maoni ni Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Lilian Liundi aliyetaka kuondolewa kwa gharama za kuchukua fomu ili kuwapa fursa wanawake wengi washiriki mchakato huo.
Alipendekeza wagombea waliowahi kushitakiwa kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia au kufanya ukatili wowote wasiruhusiwe kugombea.
Alitaka usawa wa kijinsia katika vyama vya siasa kwa kuonyesha umri, jinsia na aina ya ulemavu ili kuwa na taarifa sahihi ya watakaopitishwa kuwania nafasi mbalimbali.
Naye mwakilishi wa Chama cha Demokrasia (DP), Abdul Mluya aliitaka Serikali itoe ruzuku kwa vyama vyote vya siasa nchini hasa vile vilivyoshiriki uchaguzi kwa miaka kuanzia mitatu hadi mitano mfululizo.
Alisema kama vyama vitashindwa kushiriki uchaguzi basi vitakuwa vimejiondoa vyenyewe kwenye ruzuku na kuondoa utitiri wa vyama vya siasa nchini.
Naye katibu Mkuu wa Chama cha UDP, Swaumu Rashidi aliitaka Serikali kutoa ruzuku kwa vyama vyote vya siasa ili wasishawishike na fedha za magaidi na mafisadi ambao wana lengo la kuhatarisha usalama wa Taifa.
Malalamiko ya vyama
Akifafanua malalamiko ya baadhi ya vyama vya siasa kuhusu kunyimwa haki ya kutoa maoni, Dk Mhagama alisema nafasi ilitolewa kwa wote bila upendeleo na hadi jana vyama 10, taasisi za kidini na wadau mbalimbali wameshatoa maoni yao.
"Hakuna chama cha siasa ambacho kina umuhimu kuliko chama kingine na ndiyo maana vyama vyote vimetoa maoni yao kwa siku hizi nne bila upendeleo wa aina yoyote," alisema.
Alisema jumla ya vyama vya siasa 18 vyenye usajili na Asasi za kiraia 400, zimetoa maoni.
“Pia, taasisi za dini na watu binafsi wametoa maoni yao moja kwa moja na wengine kwa njia ya maandishi kwa siku nne ambazo kamati hiyo ilikuwa inakusanya maoni,” alisema. |
Hivi unakumbuka zamani isingewezekana kijana amekalia kiti kwenye chombo cha usafiri wakati mtu mzim | Hivi unakumbuka zamani isingewezekana kijana amekalia kiti kwenye chombo cha usafiri wakati mtu mzima amesimama?
Lakini wakati wa kula pia, ilikuwa haramu kwa mtoto kuanza kunawa kabla ya mkubwa na aghalabu wakubwa ndiyo waliokuwa wa kwanza kunawa hata baada ya kula.
Ule utaratibu wa kumsalimu mkubwa kwa kubonyea kama unapiga goti, kadhalika ilifanyika hivyo hata unapomkabidhi au kumpokea kitu, unaukumbuka?
Sio hayo tu, haikuwa rahisi kukataa maelekezo ya mzazi kwa kusema ‘sitaki’ au kuguna kunakoashiria umechoka au unagoma kutekeleza anachokwambia.
Hiyo ni mifano ya tamaduni chache kati ya nyingi zilizokuwa zinafanyika zamani kama ishara ya heshima na adabu, ambazo kwa sasa zinaendelea kupotea.
Sababu ya kupotea kwake ni kile kinachoelezwa na wahenga, kumetokea mmomonyoko mkubwa wa maadili kwa vijana, hali inayowafanya waone kuenzi tamaduni za kale ni ushamba.
“Vijana wa siku hizi wanajifanya wajuaji wa kila kitu, hata ukimwelekeza hiki atakwambia kile. Wanakwambia kufanya ya zamani ni ushamba. Kwa ufupi ni kundi lisilobebeka,” anasema mzee Marco Kindinda mkazi wa Dar es Salaam.
Hata hivyo, vijana wanasema kila kinachofanywa nao ndicho walichofunzwa na wazazi wao na walikwenda mbali zaidi wakisema “kama wazazi walipanda boga, wasitarajie kuvuna tikiti.”
“Wao walilelewa vizuri ndiyo maana wanajiona wana heshima na adabu, lakini wameshindwa kutulea kama walivyolelewa leo hii wanamlaumu nani, hivi tulivyo ndivyo walivyotufundisha, wamepanda boda wanataka wavune tikiti haiwezekani,” anasema Leons Daniel kijana anayeishi Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo, Jumatano Januari 10, 2024, Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania, Tonisiza Antonia anakiri kuwepo makosa katika malezi yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na wazazi wa kizazi cha sasa.
Anarejea malezi aliyoyapata yeye zamani, wakati mwingine alijikuta anapokosea anaadhibiwa hata na jirani na mzazi wake hakuwahi kulaumu.
“Kwanza hata nyumbani huendi kusema kama umechapwa maana ukisema watakuuliza sababu ya kuadhibiwa na hatimaye utachapwa tena,” anasema.
Anaeleza utaratibu huo ulitoa mwanya kwa kila mtu mzima katika jamii kurekebisha tabia ya mtoto yeyote, hivyo isingekuwa rahisi kukosea.
Lakini kinachofanyika sasa, anasema mtoto akiadhibiwa na asiyemuhusu, wazazi wanakwenda kuripoti Polisi kumsingizia makosa lukuki.
Makosa mengine, anasema ni kukosekana kwa utaratibu wa kuwasimulia watoto tamaduni nzuri zilizokuwa zinafanyika zamani, wakizisikia ukubwani wanaishia kuziona kama ushamba.
“Sisi tumelelewa vizuri lakini tumekuja kukosea namna ya kuwalea watoto zetu. Hatupaswi kumlaumu yeyote tujipange kukabiliana na kinachoendelea na tuone namna ya kurekebisha,” anasema.
Sambamba na mtazamo wa Tonisiza, Meneja wa Miradi wa Shirika la Mabadiliko ya Vijana Afrika (AYT), Arafat Lesheve anasema sehemu kubwa ya mwenendo wa vijana wa sasa ni matokeo ya athari hasi za utandawazi.
Anasema wengi wamejikita katika kujifunza kupitia mitandao, majukwaa ambayo hayahusishi tamaduni za kitanzania, badala yake yanafundisha usasa.
“Utandawazi umechangia wengi wanajifunza kupitia mitandao ya kijamii na inategemea humo kwenye mitandao anaangalia nini hasa,” anasema.
Licha ya mtazamo huo, Lesheve naye anatupa mzigo wa lawama kwa wazazi, akisema wengi hawajishughulishi na kuelimisha watoto kuhusu tamaduni za kale.
“Kwanza watoto wengi kwa sasa wanalelewa na mzazi mmoja ambaye mara nyingi hana muda wa kumuangalia mwanawe. Watoto wanalelewa na wafanyakazi wa nyumbani,” anasema. |
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), inatarajia kuanza utekelezaji wa mradi wa Bandari ya | Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), inatarajia kuanza utekelezaji wa mradi wa Bandari ya Bagamoyo, pale itakapokamilisha taratibu za kumpata mzabuni.
Huu ni miongoni mwa mipango iliyopangwa muda mrefu na Serikali, lakini haukuwahi kuwa katika vitendo, badala yake kila awamu ilikuja na hoja zake.
Dhamira ya utekelezaji wa mradi huo ilianza muongo mmoja na kidogo, tangu pale Serikali ilipopanga mpango wa miaka 20 wa uendelezaji bandari nchini 2019/2028.
Mpango huo pamoja na mambo mengine ulihusisha dhamira ya ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na matarajio ya kukamilika kwake ilikuwa ni mwaka 2021/22.
Hilo halikutimia, mambo yalikuwa mengi. Zabuni ilitangazwa na alipatikana mwekezaji, lakini Serikali enzi za Hayati John Magufuli ilimpinga.
Upinzani wa Serikali dhidi ya mwekezaji huyo, ulitokana na kile kilichoelezwa, mkataba wa utekelezaji wa mradi huo na uendeshaji wake unainyonya Tanzania. Kwa maneno mengine Tanzania isingenufaika na chochote na mikataba huo.
Hali hiyo ilisababisha Hayati Magufuli asitishe mikataba huo huku akitoa sababu nyingine ikiwemo masharti magumu yaliyomo katika muundo wa mkataba baina ya Tanzania na mwekezaji.
Mikataba huo uliositishwa mwaka 2019 na Magufuli, ulisainiwa mwaka 2013, kati ya Tanzania na kampuni ya China Merchant Holdings International, inayoendesha bandari ya China.
Kulingana na masharti ya mikataba huo, mwekezaji huyo alikuwa na jukumu la ujenzi wa bandari na eneo maalum la uchumi lililotajwa kuifanya Afrika Mashariki kuwa kituo cha biashara na usafirishaji.
Hayo yalipita na hatimaye hata mpango uliolenga kukamilisha ujenzi wa bandari hiyo mwaka 2022 ulipita bila hilo kutekelezwa.
Licha ya historia hiyo ya mabonde na milima ya utekelezwaji wa mradi wa bandari hiyo, kwa mtazamo wangu angalau naona dalili za ahadi hii kuwa vitendo.
Januari 9, 2024, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa alitangaza mpango wa ujenzi wa bandari hiyo ambao kimsingi ulianza tangu Novemba mwaka jana Serikali ilipotangaza zabuni kumpata mkandarasi.
Lakini kilichoelezwa naye, juzi kimeonyesha moshi mweupe katika utekelezaji huo, kwani badala ya kusubiri mwekezaji Serikali yenyewe imepanga kutekeleza kwa kuanza na gati mbili, badala ya saba zilizopangwa awali.
Lakini badala ya utekelezaji wake kuhususha na ujenzi wa eneo maalum la uchumi na biashara, kwa sasa Serikali imesema inatekeleza kwa awamu kwa maana itaanza na bandari kisha ndiyo ujenzi wa eneo hilo.
Gati zilizobakia kwa maana namba tatu hadi saba imesema itatafuta mwekezaji kutoka sekta binafsi itakayeshirikiana naye.
Ujenzi wa bandari hii kwangu ni turufu nyingine ya ukuaji uchumi wa Tanzania, kwani pamoja na yenyewe kuingiza mapato, itarahisisha huduma katika bandari nyingine nchini.
Mizigo mingi takriban asilimia 92 ya ndani na 95 ya nje iliyokuwa inahudumiwa na Bandari ya Dar es Salaam itagawanyika na hatimaye kufungua mwanya wa kuongezeka kwa shehena zaidi ambayo matokeo yake ni mapato ya kikodi na tozo kuongezeka.
Si hivyo tu, utekelezwaji wa bandari hiyo utaimarisha ushindani na bandari shindani kama Mombasa kwa kuwa, Bagamoyo ipo katika eneo la kimkakati.
Iwapo mradi huo utatekelezwa wasafirishaji watakuwa na machaguo kulingana na eneo walilopo, badala ya sasa ambapo wanalazimika kwenda katika maeneo kadhaa.
Kinachofurahisha zaidi ni ile hatua ya magati hayo mawili yanayojengwa kuwa na uwezo wa kuhudumia meli mbili kwa wakati mmoja, jambo linalotarajiwa kuongeza ufanisi zaidi.
Angalizo langu, baada ya kukamilika kwa mradi huo uundwe mkakati wa kuzitangaza bandari hizo ili zijulikane na hatimaye kutumika na wasafirishaji.
Nasema hivi kutokana na uzoefu kwamba, pamoja na Tanzania kuwa na bandari sita zinazojulikana zaidi, zipo ambazo wateja hawazifahamu jambo lililosababishwa na kutotangazwa vema sokoni.
Kile ambacho TPA inakiita makongamano ya masoko kinapaswa kiongezewe nguvu ili iwe rahisi kwa Tanzania kuzitangaza bandari zake zote.
Lakini, wakati utekelezwaji unakamilika, angalau Serikali ijitahidi au ishirikishe sekta binafsi kupata vifaa vya kutosha ili sifa za gati zilizopo zikawe na uhalisia. |
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), inatarajia kutumia takriban Sh2.1 trilioni kwa ajili | Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), inatarajia kutumia takriban Sh2.1 trilioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ili kukabiliana na ongezeko la mizigo bandarini.
Fedha hizo ni kwa ajili ya upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam kwa kujenga gati nne, kadhalika ujenzi wa gati mbili katika mradi wa Bandari ya Bagamoyo.
Kulingana na TPA, kumekuwepo na ongezeko la mizigo katika bandari hasa ya Dar es Salaam kama takwimu za Julai hadi Desemba mwaka 2023 zinavyobainisha.
Kwa mujibu wa takwimu hizo, mamlaka hiyo ilikuwa na lengo la kuhudumia meli 792, lakini imezihudumia 979, sawa na asilimia 123.6.
Kwa upande wa makasha yaliyohudumiwa ni 595,940, ikiwa ni zaidi ya lengo la kuhudumia makasha 495,600, sawa na ufanisi wa asilimia 102.8.
Licha ya ahadi ya maboresho ya bandari hizo, wadau wameshuku uwekezaji mbalimbali uliowahi kufanyika lakini bado bandari zinakabiliwa na uhaba wa vifaa.
Hayo yalielezwa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa utendaji wa mamlaka hiyo.
Gati nne bandari Dar
Katika maelezo yake, Mbossa alisema mamlaka hiyo inatarajia kupanua bandari ya Dar es Salaam kwa kuongeza gati nne na hivyo kufanya jumla ziwe 15.
Kuongezwa kwa gati hizo namba 12 hadi 15, alisema kunatokana na ukweli kwamba bandari hiyo inahudumia asilimia 92 ya mizigo yote inayosafirishwa kwa bandari nchini na asilimia 95 ya mizigo ya nje.
“Kumekuwa na ongezeko la meli zinazohudumiwa katika bandari ya Dar es Salaam kutokana na kuimarika kwa sera za kiuchumi, kiuwekezaji na diplomasia,” alisema.
Kulingana na Mbossa, gati hizo nne zitakuwa na uwezo mkubwa zaidi ya zile za sasa na kwamba thamani ya ujenzi wake kwa gati moja ni takriban Sh350 bilioni.
Ujenzi bandari Bagamoyo
Mradi mwingine unaotekelezwa kukabili ongezeko la mizigo, mkurugenzi huyo alisema ni ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo utakaohusisha gati mbili za awali zitakazokuwa na uwezo wa kuhudumia meli mbili kwa wakati mmoja.
Meli zitakazohudumiwa katika magati hayo, kwa mujibu wa Mbossa zitakuwa na uwezo wa kubeba makasha 25,000 ambayo ni tofauti na zile zinazohudumiwa katika Bandari ya Dar es Salaam zenye uwezo wa kubeba makasha 8,000.
“Gati mbili za awali tutajenga wenyewe, lakini nyingine tunatarajia kushirikiana na sekta binafsi kwa kuwa uwekezaji katika miradi ya bandari unahitaji fedha nyingi,” alisema.
Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji, alisema TPA imeamua kutekeleza mradi huo kwa awamu, badala ya mpango wa awali uliotaka utekelezwaji wake uhusishe na ujenzi wa eneo maalum la uchumi.
Alieleza kwa sasa wameamua kuanza na ujenzi wa bandari hiyo kisha eneo la uchumi litafuata, ili kuharakisha urahisi na unafuu wa huduma katika bandari nchini.
"Tumeona haja ya kuharakisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kutokana na hali iliyopo, kwamba baadhi ya meli haziwezi kuhudumiwa na bandari ya Dar es Salaam kutokana na magati kuwa madogo," alisema.
Hata hivyo, Mbossa alibainisha matarajio ya kukamilika kwa mradi huo ni mwaka 2028 na kwa sasa mchakato wa kumpata mzabuni unaendelea.
Alisema bandari hiyo ya Bagamoyo inatarajiwa kuwa na kina chenye urefu wa mita 18, zaidi ya Dar es Salaam yenye kina cha mita 14.5.
Mradi mwingine unaotekelezwa, alisema ni ujenzi wa eneo maalum la kupakulia mizigo ya mafuta inayokwenda sambamba na ujenzi wa matenki ya kuhifadhia mafuta hayo.
Kadhalika, alieleza ujenzi wa eneo maalum la kupakulia mizigo Kurasini jijini Dar es Salaam, ili kupunguza msongamano wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam.
Eneo hilo, awali lilimilikiwa na Mamlaka ya Eneo Huru la Uwekezaji kwa Mauzo Nje (EPZA) kisha baadaye uamuzi ulifanyika na kukabidhiwa kwa TPA.
Changamoto
Pamoja na kuvuka lengo la utoaji huduma mbalimbali katika bandari hiyo, Mbossa alieleza uwepo wa changamoto ya miundombinu ya reli kwa ajili ya kutoa mizigo bandarini.
Alieleza miundombinu ya reli iliyopo ina uwezo wa kutoa mizigo kutoka katika bandari hiyo kwa asilimia tatu pekee, huku mingine ikihudumiwa na malori.
“Miundombinu isiyotosheleza ya reli na barabara inapunguza mizigo na reli iliyopo inaondoa asilimia tatu tu ya mizigo yote bandarini,” alisema.
Hata hivyo, alifafanua matumaini ya kutatuliwa kwa changamoto hiyo ni kukamilika kwa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR), inayotarajiwa kupunguza mizigo bandarini.
Changamoto nyingine ni kuharibika mara kwa mara kwa midaki inayotumika kuskani mizigo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo magari kugonga.
“Ikiharibika inasababisha shughuli zisimame na unaposinamisha siku moja maana yake unachelewesha mizigo inayohudumiwa katika bandari zetu," alisema.
Kuharibika kwa mitambo mingine, alisema kunatokana na ukweli kwamba, mingi imenunuliwa kati ya mwaka 2009 na 2012 na juhudi zinafanyika kuhakikisha mitambo zaidi inapatikana.
"Tuna wadau tumeingia nao mikataba na tunasubiri watakaokuja watakuja na mitambo, ndiyo maana tumeshirikiana na sekta binafsi," alisema.
Mvua za El-Mino ni changamoto nyingine iliyotajwa na Mbossa, akisema inaponyesha inasababisha shughuli ya upakuaji wa baadhi ya mizigo kama ngano kusimama.
Kadhalika, alieleza baadhi ya magati yanatumika kwa shughuli za kijamii, zikiwemo za kijeshi, zinazofanya utafiti na oparesheni mbalimbali.
Kwa kuwa mamlaka hiyo inahudumia bandari sita zikiwemo tatu za maziwa makuu na nyingine za mwambao wa bandari ya Hindi, alisema maboresho hayo yamehusisha na bandari nyingine.
Mathalan, kwa bandari ya Tanga alisema kina kimeongezwa kutoka mita tatu hadi 13, lakini Mtwara gati mpya zimejengwa na vifaa vya kisasa.
Mengine yaliyofanyika, alisema ni kuwa na tozo shindani, ujenzi wa ofisi nje ya nchi na sasa zipo sita, uhifadhi wa siku 30 wa mzigo katika bandari ya Kwala bila kutozwa gharama za kuutunza.
Mengine, alisema wamefanikiwa kuhakikisha mifumo ya TPA na TRA inasomana, jambo lililowahi kulalamikiwa na Hayati John Magufuli.
Mtazamo wa wadau
Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA), Edward Urio alisema licha ya maboresho mbalimbali yaliyofanyika, bado kuna upungufu wa vifaa katika bandari nchini.
“Uwekezaji umefanyika lakini bado vifaa havipo vya kutosha, hili ni jambo tunalopaswa kuliangalia ili kuongeza ufanisi na kuvutia wateja wengi,” alisema.
Hata hivyo, alieleza uwepo wa changamoto katika kuzitangaza baadhi ya bandari, mathalan ya Tanga hali inayosababisha zisitumiwe na wasafirishaji ilhali zipo katika jiografia shindani.
“Wengi hawaelewi kama kijiografia Bandari ya Tanga ndiyo bandari shindani kwa bandari ya Mombasa, kwa maana ya ujirani na eneo ulilopo,” alisema.
Kinachohitajika, alisema ni kuitangaza ili wasafirishaji waijue na kuitumia hatimaye kuongeza mapato ya nchi.
Kadhalika, Urio alipongeza maboresho yaliyofanyika katika bandari ya Mtwara, akisema kwa sasa imekuwa ikihudumia mizigo kuizidi ya Tanga.
Mtafiti na mshauri wa masuala ya kiuchumi, Thobias Shija alisema matokeo ya maboresho yoyote katika bandari ni huduma kuwa bora na ufanisi kuongezeka.
Hayo, alisema yatachagiza idadi kubwa ya wateja katika bandari husika, jambo ambalo matokeo yake ni kuongezeka kwa mapato yanayotokana na tozo na kodi zinazolipwa na wateja hao.
“Mapato ya kikodi na tozo yataongezeka kwa sababu wateja watakuwa wengi. Wafanyabiashara mara nyingi wanapenda huduma za haraka na rahisi. Kwa hiyo wengi watavutika,” alisema. |
Kama ulidhani mfanyakazi wa nyumbani ‘house girl’ ni kiumbe anayestahili majukumu makubwa bila haki, | Kama ulidhani mfanyakazi wa nyumbani ‘house girl’ ni kiumbe anayestahili majukumu makubwa bila haki, sheria inamlinda.
Hii inatokana na uhalisia kwamba, waajiri wengi wa wafanyakazi wa nyumbani, huwatumikisha kazi bila kufuata utaratibu na aghalabu ni kazi inayodharaulika.
Kwa taarifa yako, haki aliyonayo mtumishi wa umma na mfanyakazi wa taasisi yoyote, ndiyo aliyonayo mfanyakazi wa nyumbani, kulingana na mkataba namba 189 unaolenga kukuza kazi za staha kwa wafanyakazi wa majumbani.
Katika mkataba huo ambao Tanzania ipo mbioni kuuridhia, vipo vipengele vinavyoonekana kuwapa wakati mgumu waajiri kuvitekeleza, kutokana na mazoea waliyonayo juu ya kuishi na wafanyakazi hao.
Miongoni mwa vipangele hivyo ni haki ya faragha kwa mfanyakazi huyo, inyohusika kupewa chumba chake. Lakini uhalisia wafanyakazi hawa hulazwa na vijana wa waajiri au wakati mwingine sebuleni na koridoni.
Kipengele hicho kinamuibua mmoja wa waliowahi kuwa waajiri wa mfanyakazi wa nyumbani, Mary Elia anayesema vipato duni vinawasababisha kushindwa kumudu kupanga zaidi ya chumba kimoja au viwili.
“Hivyo kwa hali hii, ni wazi kwamba msichana atalala tu na watoto hamna namna kwani kama una vyumba viwili , kimoja utalala na mme wako na kama hauna mume basi utalala na mtoto au watoto wako.
“Kile kinachobaki ambacho mara nyingi ndio hutumika kama jikoni, sebuleni, ndipo atalala dada,”anasema Marry.
Wakati hali ikiwa hivi, Ofisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Dar es Salaam, Joyce Maketa anasema ni hatari sana kuwalaza watoto na dada, kwa kuwa wote wamelelewa katika namna tofauti.
“Tumekuwa tukishuhudia baadhi ya kesi za wafanyakazi wa majumbani wakiwafanyia vitu vibaya watoto wa matajiri wao ikiwemo mambo ya kishirikina, kuwalazimisha kufanya nao ngono bila kujali umri wao na mwisho wa siku kuwaambukiza magonjwa ya zinaa hivyo ni vema dada akawa na chumba chake sio kwa usalama wake tu bali na watoto wako pia,”alisema.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi majumbani, Zanini Othuman anasema kumlaza mfanyakazi huyo sebuleni inamshushia thamani yake, pia ni rahisi kufanyiwa vitendo vibaya.
“Hivyo mfanyakazi wa majumbani naomba waajiri waelewe kwamba anapaswa kuwa na chumba chake tena chenye kitasa kizima kwa kuwa tumeshuhudia wengi vitasa vya milango ya wafanyakazi hawa huwa vinakuwa vibovu wakati wote jambo ambalo sio sawa,” anasema Zanini
Likizo yenye malipo
Likizo yenye malipo ni sehemu ya vipengele hivyo, kikiwataka waajiri kuwalipa wafanyakazi hao wanapokwenda likizo, huu nao ni mtihani mwingine kwa waajiri.
Nasra Selemani amesema ni muhimu jambo hilo lizingatiwe, kwa kuwa mara nyingi mfanyakazi wa majumbani hapewi likizo hadi anaamua kuongopa ilia pate mwanya wa kurudi kwao.
“Tunaomba suala la likizo lizingatiwe, kwani hata sisi ni binadamu kuna muda tunahitaji kupumzika, hivyo kama nyie mnavyopewa likizo ofisini kwenu nasi mnapaswa kututendea hayo pia,” anasema Nasra.
Lakini James Urio wa Mbezi Dar es Salaam amesema ni vigumu kumlipa mfanyakazi huyo likizo kwa kuwa anakuwa nje ya sehemu ya majukumu yake ya kazi.
Wakati Urio akieleza hivyo, Mkuu wa Idara ya Sheria wa Chama cha wafanyakazi wa Majumbani Hifadhi, Mahotelini, Huduma za jamii na Ushauri (CHODAWU ), Asteria Mathias amesema kama mwajiri anaona kumpa likizo mfanyakazi atapoteza, anapaswa kutafuta mbadala ili mwingine akapumzike.
Ashura Imamu, anasema kumpa mfanyakazi hela ya likizo ni vigumu kutokana na ukweli kwamba hata hao wajiriwa wengi wanaopewa likizo maofisi hawapati haki hiyo.
Mapumziko ya wiki
Kipengele kingine ni mfanyakazi wa nyumbani anatakiwa kupewa siku moja ndani ya wiki kwa ajili ya kupumzika kwa saa 24.
Hiyo siku, mwanasheria wa Chodawu, Wagala Shungu amesema mfanyakazi huyo hapaswi kushika chochote kinachohusiana na kazi hadi saa hizo zitakapokamilika.
Amesema kama kutakuwa na sababu za msingi za kutopumzika, anapaswa kulipwa malipo ya ziada.
Mkazi wa Magomeni, Naomi Joseph amesema itawezekana kama waajiri watapewa elimu ya haki za wafanyakazi hao.
“Elimu tu hapa naona ndio muhimu, kwani bado wafanyakazi hawa watu waliwaweka daraja la chini kiasi cha kuwanyima haki zao na kuonekana ni watu wanaotakiwa kufanya kazi saa zote, tuendelee kupeana elimu bila kuchoka,” amesema Naomi.
Posho saa za ziada
Kwa mujibu wa Chodawu, unapomfanyisha kazi mfanyakazi wako wa nyumbani nje ya saa za kazi zinazojulikana kiserikali unapaswa kumlipa.
Kwa mujibu wa sheria za kazi, saa za kufanya kazi ni tisa. Hata hivyo sheria hii haitekelezwi na waajiri wengi.
Kwa mujibu wa Chodawu, hata pale mfanyakazi huyo anapoamka usiku kumfungulia mume wa bosi wake mlango, anapaswa kumlipa kwa kuwa ni nje ya muda wa kazi.
“Utakuta mama kalala, mume anaporudi msichana wa kazi ndio anaenda kufungua geti au mlango, hii ni sawa na kumfanyisha kazi ya ziada, hivyo unapaswa kumlipa, “ amesema Wagala ambaye ni mwanasheria wa Chodawu.
Mafao
Kama ulidhani mfanyakazi wa ndani hana haki ya mafao, hii inakuhusu. Kisheria wafanyakazi hawa wanapaswa wanapaswa kuwa na mafao, ingawa wengi hulipwa fedha mkononi.
Pia kikwazo kingine katika kuchangia kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, ni kima chao cha chini cha mshahara wengine huwa kidogo, kisichostahili kukatwa.
Kwa mara ya mwisho kima cha chini kilichotangazwa kwa wafanyakazi hao wa majumbani ni Sh60,000 kwa wale wanaoishi nyumbani kwa mwajiri.
Hivyo akikatwa Sh30,000 ni wazi kwamba atabakiwa na Sh30,000 fedha ambayo hawezi haitatosheleza mahitaji yake ya msingi kwa mwezi.
Mwisho.
Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) imesema majeruhi wengi wa bodaboda wanaofikishwa katika taasisi hiyo wana mivunjiko mikubwa na ndiyo inayosababisha gharama kubwa za matibabu.
Kulingana na MOI, uchunguzi wa hivi karibuni umebaini kwa siku taasisi hiyo inapokea majeruhi 20 hadi 25.
Hayo yameelezwa hivi karibuni na Daktari bingwa mbobezi wa Mifupa MOI, Dk Joseph Mwanga wakati akielezea matukio yanayohusisha majeruhi wa bodaboda wanaopokelewa kwenye taasisi hiyo.
“Majeruhi huvunjika vibaya sana, mtu huyu atatumia muda mwingi na gharama kubwa kujitibia, wakati nwingine kama sio kifo basi anaweza asirejee katika hali yake ya kawaida…kundi hili la bodabda na bajaji ndilo linaloongoza kwa ajali,” amesema.
Amesema asilimia 60 ya majeruhi hao wanatokana na bodaboda na wanaopokelewa katika kitengo cha dharura MOI.
Kwa mujibu wa takwimu za taasisi hiyo, asilimia 30 ya majeruhi hao wanatokana na ajali za gari na asilimia 10 ni ajali nyingine.
“Ajali hizi za pikipiki zinaongoza kusababisha majeruhi na wanaume ndilo kundi linaloathirika zaidi kwa asilimia 70, majeruhi wengi wa bodaboda hupata mivunjiko mikubwa ya mifupa hali inayochangia ukubwa wa gharama za matibabu,” amesema.
Dk Mwaga amesema kwa miaka 18 iliyopita kitengo cha dharura cha MOI kilikuwa kinapokea majeruhi watatu hadi watano kwa siku, ukilinganisha na sasa ambapo majeruhi 20 hadi 25 hupokelewa kwa siku.
Septemba 29, mwaka jana katika maadhimisho ya siku ya moyo, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisema changamoto inayowakabili wanaofanya mazoezi barabarani ni kupoteza maisha kwa ajali za bodaboda.
Ili kutatua changamoto hiyo amesema atawasilisha ombi kwa Waziri Mkuu Kassim Majliwa ili barabara zinazojengwa ziwe rafiki kwa wananchi wanaofanya mazoezi.
Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria watu milioni 1.9 hupoteza maisha kutokana na ajali za barabarani na ndizo zinazoongoza kwa vifo vya watoto na vijana kuanzia miaka mitano hadi 29.
Kulingana na shirika hilo, asilimia 92 ya vifo vinavyotokea barabarani ni katika mataifa yanayoendelea na zaidi ya nusu ya waathirika wa ajali hizo ni watumiaji wa barabara.
WHO inasema ajali za barabarani hutumia asilimia tatu ya pato la taifa kwa mwaka. |
Imepita miongo mitatu bila mafanikio ya kutamatika kwa mgogoro wa ardhi kati ya Bakari Ismaili (75) | Imepita miongo mitatu bila mafanikio ya kutamatika kwa mgogoro wa ardhi kati ya Bakari Ismaili (75) dhidi ya Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Babati.
Mzizi wa mgogoro huo ni madai ya Ismaili kwamba alinyang’anywa eneo hilo la ekari tatu analodai lilikuwa la kwake mwaka 1994 na likakabidhiwa kwa kanisa.
Hata hivyo, kanisa hilo limeyakana madai hayo, likisema Ismaili alishashitaki zaidi ya mara tatu mahakamani, lakini zote alishindwa.
Akisimulia madai ya kunyang’anywa eneo hilo, Ismaili amesema mchakato ulianza kwa kuandikiwa barua kuhusu kuchukuliwa kwa eneo hilo na Ofisa Maendeleo wa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Babati wa wakati huo.
Barua hiyo, amesema aliandikiwa Mei 27, 1994 na ndani yake ilieleza eneo hilo linakabidhiwa kanisa ili kujengwa kituo cha maendeleo ya vijana.
Kwa mujibu wa Ismaili, alilipata eneo hilo mwaka 1974 wakati wa oparesheni ya vijiji na kuliendeleza kwa kupanda mazao ya kudumu ikiwamo miti na migomba.
"Nilinyang'anywa kienyeji mwaka 1994, Mei 26, 1994 niliandika barua ya malalamiko kwa mkurugenzi mtendaji wilaya ambaye alinijibu kupitia afisa maendeleo wa ardhi (Mzava).
"Barua ile yenye kumbukumbu namba GEN/BBT/VOL.IV/84 ya Mei 27, 1994 ilidai kutambua eneo hilo lenye mashina 50 ya migomba na miti 100, ikisema ni eneo la kanisa.
Ameongeza: "Juni 6, 1994 nilipokea barua ya uthamini wa mimea yangu ambayo barua ile ilidai mimea yangu ipo kwenye eneo la kanisa.
Amesema barua ilimjulisha mthamini wa serikali atafika Juni 8, 1994 ili kuthaminisha mimea yake ya kudumu hivyo awepo kwenye eneo hilo saa 5:00 siku inayofuata.
"Nilikwenda kama nilivyoelekezwa lakini mthamini hakutokea na hakuna kilichoendelea tena, baadae nilipeleka malalamiko yangu kwa mkuu wa wilaya ya Babati na mkuu wa mkoa wa Arusha kabla hujagawanywa (sasa ni Manyara) huko nako sikupata ushirikiano,” amesema.
Amesema aliendelea kuhangaika kutafuta hki yake hadi Aprili, 23, 2021 alipomuandikia barua ya malalamiko Kamishna wa ardhi wa mkoa.
"Nilijibiwa kwamba Kamishna wa ardhi msaidizi anaitwa Msafiri amemwandikia mchungaji kiongozi wa kanisa yenye kumb namba LD/MNR/01/VOL.3/49 ya Julai 22, 2021, lakini hadi sasa sijapata msaada.
"Nilipeleka malalamiko yangu kwa waziri wa Ardhi (Jery Silaa), Agosti 10, 2022 katika kufuatilia ilipofika Februari 12, 2023 hoja yangu ilipewa usajili namba ST-006-007-05722, baada ya hapo hakuna kilichoendelea, zaidi niliishia kuwekwa lock up (mahabusu) ili nisiendelee kutafuta haki yangu," amesema.
Mchungaji wa Dayosisi hiyo, Frank Chikoti amesema aliukuta mgogoro huo mwaka 2012 alipofika eneo hilo kwa ajili ya kazi ya uchungaji na wameshashitakiwa katika baraza la ardhi mara mbili na zote Ismaili alishindwa.
"Tumewahi kusuluhishwa na wakuu wa wilaya watatu wa hapa Babati kwa nyakati tofauti akiwamo huyu wa sasa Lazaro. Kimsingi huyo mtu ametushtaki sio mara moja na kashindwa zote.
“Kuna wakati alivamia kwenye eneo hilo wakamfunga miezi sita, alipotoka akafungua kesi akashindwa, akafungua tena akashindwa kanisa lina vielelezo vya umiliki," amesema.
Mchungaji huyo amesema umiliki wa eneo hilo waliupata mwaka 1994 walipokabidhiwa na mtu aliyemtaja kwa jina la Samson Agunda.
"Sehemu chache ya eneo iliyokuwa imesalia Halmashauri ilisema tuwafidie wenye maeneo yao, tukafanya hivyo wakaondoka, japo wakati huo sikuwa mchungaji hapo, lakini vielelezo vya nyaraka hizo zipo na mmoja wa waliofidiwa alikuwa ni jirani wa huyo mzee Bakari.
"Huyo mzee alitia saini kwa mwenzake akipokea malipo, leo hii anakuja kudai kiwanja ni chake, hayo ndiyo yameleta utata ingawa kiwanja ni mali halili ya kanisa na lina haki miliki,” amesema. |
Huenda tabu ya usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam imebakiza muda mchache, baada ya Serika | Huenda tabu ya usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam imebakiza muda mchache, baada ya Serikali kufungua milango ya ushirikiano na sekta binafsi katika uwekezaji wa ujenzi wa miundombinu ya reli na utoaji huduma za usafiri huo.
Kabla ya kufunguliwa milango hiyo, mwekezaji katika miundombinu hiyo na huduma ilibaki kuwa Serikali pekee, jambo lililoisababishia mzigo na hatimaye kutoa huduma zisizoridhisha.
Katika mazingira hayo, usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam, ulikosa uhakika, huku abiria wakilalamikia uchakavu wa miundombinu na treni zenyewe.
Lakini, hii si mara ya kwanza Serikali kutangaza kumsaka mwekezaji, awali 2014 ilimtangaza Dk Robert Shumake kutoka Marekani, kuwa mwekezaji atakayeleta treni za kisasa kwa ajili ya kuhudumia Jiji la Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi wa wakati huo, Dk Harrison Mwakyembe alisema uwekezaji huo utamgharimu Dk Shumake Sh40 bilioni, jambo ambalo hadi leo halijafanikiwa.
Hatimaye hatua ya ushirikiano wa Serikali na sekta binafsi (PPP) iliyotangazwa jana, ndiyo tumaini la kukoma kwa shuruba za usafiri huo katika Jiji la Dar es Salaam.
Taarifa kuhusu mpango huo wa PPP, ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa mbele ya Waziri wa Ardhi, Miundombinu, Usafirishaji na Utalii wa Japan, Kokuba Konosuke waliokutana kwa mazungumzo ya ushirikiano katika uwekezaji.
Katika hotuba yake ya ufunguzi, Profesa Mbarawa alisema Serikali imepanga kushirikiana na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ukiwemo wa reli katika Jiji la Dar es Salaam.
Kulingana na waziri huyo, ushirikiano huo utahusisha ujenzi wa mtandao wa reli mpya na upatikanaji wa treni kwa ajili ya usafirishaji wa abiria katika eneo hilo.
“Wajapan tunawafahamu ni kampuni ambazo zimekuwa zikifanya kazi kwa kuzingatia ubora, tunatarajia kuziona zikitumia fursa hii," alisema.
Akilifafanua hilo, Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa alisema utafiti umeshafanyika katika eneo la Tegeta-Mwenge-Ali Hassan Mwinyi-Katikati ya Jiji na Bakhresa kisha Uwanja wa Ndege.
“Watu wengi wanavutiwa kuwekeza katika eneo hilo, kwa sababu wamefanya utafiti na kuona ni njia inayotumika na watu wengi, kwa hiyo tungependa sekta binafsi ndiyo iingie na sio Serikali iweke fedha zake,” alisema.
Alifafanua: “Huko duniani reli za mijini zinakuwa za halmashauri lakini nafikiri majiji yetu au halmashauri zetu hazijafikia hatua hiyo, ndiyo maana TRC tunaingia.”
Kwa mujibu wa Kadogosa, kuna dalili nzuri juu ya mwamko wa wawekezaji kujenga reli katika eneo hilo, kutokana na idadi kubwa ya watu jijini Dar es Salaam.
“Tunatarajia mwaka 2030 watu watakaokuwa Dar es Salaam watafikia milioni 10, huwezi kuwasafirisha wote kwa basi lazima uwe na treni ndiyo maana tunakaribisha sekta binafsi,” alisema.
Alipoulizwa kwa undani kuhusu mradi huo ikiwemo lini utaanza na iwapo kuna mwekezaji aliyepatikana tayari, Kadogosa alisema asingependa kueleza kwa undani kwa kuwa bado mambo hayajakamilika.
Mbali na Dar es Salaam, alisema usafiri huo wa treni unatarajiwa kutumika katika Majiji mengine kama Dodoma, Mbeya, Mwanza na Arusha ambako tayari utafiti umeshafanyika.
“Hata kama hatutajenga leo, ilimradi tujue ni maeneo gani reli itapita baadaye huko watapatikana wawekezaji watajenga katika majiji mengine,” alisema.
Katika hatua nyingine, alisema kampuni za Tanzania, Mohammed Enterprises, Bakhresa Group na GSM Group zimeonyesha nia ya kushirikiana na Serikali katika kuwekeza kwenye kutoa huduma za treni nchini.
“Hawa wameonyesha nia lakini kuna taratibu za kisheria, wakionyesha nia haimaanishi kesho jambo linakuwa hapana. Kuna taratibu zinafuatwa baadaye tutawataarifu hatua zilizofikiwa,” alisema.
DP Word kuanza mwaka huu
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Plasduce Mbossa alisema mwaka huu kampuni ya Dubai Port World (DP World), inatarajiwa kuanza shughuli zake katika bandari ya Dar es Salaam.
Kampuni hiyo iliyowekeza katika baadhi ya magati kwenye bandari hiyo, ilisaini mikataba ya utekelezaji wa kazi Oktoba 23, mwaka huu.
Kinachofanyika sasa, Mbossa alisema ni makabidhiano ya eneo ambalo awali shughuli zake zilikuwa zikiendeshwa na TPA na sasa zitafanywa na DP World.
Pamoja na makabidhiano hayo, alieleza michakato mingine pia inaendelea ikiwemo ya kisheria inayohusisha kuanzishwa kwa kampuni, upatikanaji vibali na ajira.
“Siwezi kusema ni tarehe ngapi wataanza kazi kwa sababu kuna taratibu za makabidhiano zinaendelea, lakini mwaka huu wataanza uendeshaji,” alisema.
Katika hotuba yake, Waziri wa Ardhi, Miundombinu, Usafirishaji na Utalii wa Japan, Kokuba Konosuke alisema kuna miradi mingi iliyotekelezwa na Wajapan nchini Tanzania.
"Tutajadiliana kuhusu mwaliko wa kuja kuwekeza katika miundombinu ya reli na bandari Tanzania, ili kujua maeneo tutakayowekeza," alisema. |
Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo amesisitiza | Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo amesisitiza kuzingatiwa kwa maoni ya wadau kuhusu miswada ya sheria za uchaguzi, akisema jambo hilo lisifanyike kisaniisanii.
Katika kulitekeleza hilo, amewaonya wabunge na Serikali wasicheze na maoni ya wananchi, huku wakiwataka kuhakikisha Tanzania inakuwa na amani, mshikamano, maridhiano na iwe nchi ambayo wananchi wakitoa maoni yao yanaheshimiwa.
Kauli ya Askofu Shoo inakuja zikiwa zimepita siku mbili tangu Kamati za Bunge zianze kupokea maoni ya wadau Januari 6, mwaka huu, shughuli inayotarajiwa kukamilika Januari 10.
Miswada hiyo inahusisha ule wa sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2023, Sheria ya tume ya uchaguzi, sheria ya vyama vya siasa na muswada wa sheria za marekebisho ya sheria mbalimbali (Na5 bill 2023), ambayo kwa mara ya kwanza ilisomwa bungeni Novemba 10, mwaka jana.
Hata hivyo, kauli hiyo ya Askofu Shoo ni kama inakoleza wino kwenye kile kilichowahi kuelezwa na Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge Ng’ara, Severine Niwemugizi aliyetaka wanaosimamia kazi hiyo wawe na nia njema.
Askofu Shoo alitoa kauli hiyo mkoani Iringa jana, alipohutubia baada ya ibada maalum ya kuwekwa wakfu na kuingizwa kazini Askofu mteule, kutokea Usharika wa Mafinga, Anthony Kipangula na msaidizi wake, Askofu Kefa Ulula.
“Tunaomba na tunatoa wito, maoni haya yanayotolewa na wadau tukiwemo viongozi wa dini, naomba yatiliwe maanani yaheshimiwe na yafanyiwe kazi, hilo ndilo ombi langu,” alisema.
Alisema kinachotakiwa ni Tanzania yenye amani, mshikamano, maridhiano na iwe nchi ambayo wananchi wakitoa maoni yao kwa kile wanachoona ni mwelekeo na wanachotamani nchi yao iwe kiheshimiwe.
“Naomba sana zoezi la kupokea maoni, lisifanyike kisaniisanii hilo ndilo naloomba, fanyeni kwa dhati. Tutabarikiwa kama nchi,” alisema.
Katika kulitekeleza hilo, Askofu Shoo aliwataka wabunge wasimame katika nafasi yao ya kuwawakilisha wananchi.
Tume huru
Hata hivyo, Askofu Shoo alidokeza katika miswada hiyo kuna jambo moja aliloliita ndiyo sauti ya viongozi wa dini na wadau ambalo ni upatikanaji wa tume huru ya uchaguzi.
“Kwa sababu hatutaki mambo ya 2020 yajirudie, tumesema sauti ya pamoja inasema hivi na nilisikiliza viongozi wa dini na wadau mbalimbali.
“Moja ya mambo ambayo tunawaomba muyaridhie muone kwamba yanaingia katika sheria hii ya uchaguzi ni jambo la kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi,” alisema.
Ingawa haitawafurahisha wengine, Askofu Shoo alisisitiza umuhimu wa hilo kutekelezwa, akifafanua ni vema yale yanayoonekana kwa nadharia yakafanyike.
Agusia makundi
Alitumiwa jukwaa hilo, kuwataka wasaidizi wa Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha wanamsaidia kwa dhati na uaminifu ili kufikia adhma tarajiwa.
“Sasa mmesema tuwaonye, natoa wito kwa wale wote wasaidizi wa mheshimiwa Rais kama wewe (Jenister Mhagama) tunawaomba mumsaidie Rais wetu kwa dhati, kwa uaminifu kufikia adhma hii.
“Sio kuunda makundi ya kumkwamisha na hapa tunawaonya kwa sababu tunaona. Sio makundi ya kumkwamisha kwa maslahi binafsi. Mama anaiangalia Tanzania anasema sio ya leo tu wala ya kesho bali ya miaka mingi ijayo,” alisema.
Alitaka utendaji wao usiangalie mwaka 2025 (wakati wa Uchaguzi Mkuu), bali wanaangalia mbele zaidi juu ya kizazi kinachokuja cha Tanzania.
Alimsifu Rais Samia kuwa kiongozi anayetambua nafasi ya dini mbalimbali katika jamii anayoiongoza na kwamba wataendelea kumuombea.
“Rais Samia anapaswa kuendelea kuombewa kwa kuwa anazidi kujidhihirisha kwamba sio tu mchamungu pia ana nia ya dhati ya kuimarisha maridhiano na mshikamano nchini kwa ajili ya maendeleo endelevu,” alisema.
Jenister: Ukuaji wa maadili
Akisoma hotuba kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Jesnista Mhagama alisema kuanzishwa kwa Dayosisi ya KKKT Mufindi ni ishara ya ukuaji wa kijamii, kiuchumi na kimaadili.
“Huwezi kupata washirika wengi kama maadili yao mabovu. Kwa hiyo pamoja na kukuwa kwa uchumi, tunapaswa kuwapongeza watu wa Iringa kwani kuna ukuaji mkubwa wa kila sekta,” alisema.
Alieleza jambo hilo linatazamwa kama msukumo wa utashi, weledi na uzalendo utakaokuwa chemchem ya maendeleo ya taifa likiwa na misingi bora ya maadili.
“Kukuwa kwa imani katika jamii kuna mchango na ukuaji wa maadili," alisema.
Kwa mujibu wa Jenister, jamii nyingi kwa sasa zinakabiliwa na changamoto za mmomonyoko wa maadili, lakini kwa kuzingatia imani, mila na desturi njema hayo yatakoma.
Akizungumza baada ya kusimikwa kuwa kiongozi wa dayosisi hiyo, Askofu Anthony Kipangula alisema ni muhimu kuwepo ushirikiano kati ya Serikali na Kanisa katika kutoa elimu ya kujitegemea kwa vijana.
Kufanya hivyo, alieleza kutasaidia kupunguza idadi kubwa ya vijana wazururaji.
“Tumeanza kufundisha vijana kutumia fursa ya kupanda miti ya parachichi na mbao ili kujikwamua kiuchumi na Dayosisi imeanza kufanya kazi hiyo ili kuonyesha mfano,” alisema.
Alitumia jukwaa hilo, kueleza changamoto ya miundombinu ya barabara katika Wilaya ya Mufindi, akisema inakwanza usafirishaji wa mazao ya wakulima katika eneo hilo.
“Changamoto ya barabara ikitatuliwa uchumi utakuwa kwa kasi. Wakazi wa eneo hili wengi wamejikita katika kilimo cha miti, chai na wote wanachokilalamikia ni uwepo wa barabara itakayowawezesha kusafirisha mazao yao kwa haraka,” alisema.
Kuhusu mafanikio ya dayosisi, alisema wameongeza sharika na kufikia 34 na wana wachungaji 45 kwa ajili ya huduma, huku wainjilisti wakiwa 272.
“Tulifanikiwa kujenga Sekondari ya Wasichana kwa michango ya waumini na inafanya vizuri sana katika ngazi ya Wilaya mara nyingi ni ya kwanza na huwa inafanya vizuri kimkoa na kitaifa,” alisema.
Alipopewa fursa ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Halima Dendego alifafanua kuhusu barabara za eneo hilo, akisema zinajengwa kwa kiwango cha lami.
Kilichofanyika
Kilichofanyika katika shughuli hiyo ni kuzinduliwa kwa Dayosisi ya KKKT Mufindi ambayo, Askofu Kipangula amesimikwa kuwa kiongozi wake.
Kulingana na kanisa, dayosisi ni eneo fulani linalokuwa chini ya utawala wa askofu na kuzinduliwa kwa Mufindi kunaifanya KKKT kuwa na jumla ya dayosisi 25.
Mbali na askofu Kipangula kuwa kiongozi wa dayosisi hiyo, Askofu Kefa Ulula amesimikwa kuwa msaidizi wake. |
Hatua ya bandari ya Dar es Salaam kuwa chaguo la wawekezaji, imetajwa kuchagizwa na maboresho ya miu | Hatua ya bandari ya Dar es Salaam kuwa chaguo la wawekezaji, imetajwa kuchagizwa na maboresho ya miundombinu yaliyofanyika na ujuzi wa wafanyakazi.
Vingine vinavyowavutia wasafirishaji kutumia Bandari hiyo kwa mujibu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), ni uwepo wake katika jiografia sahihi na usalama wa mizigo.
Kulingana na TPA, huduma bora katika bandari hiyo ndizo zinazoifanya itumike kusafirishia vifaa mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ikiwemo ya Reli ya Kisasa (SGR).
Hayo yalibainishwa jijini Dar es Salaam jana na Meneja wa Shehena ya Mizigo Mchanganyiko katika Bandari ya Dar es Salaam, Abel Garlus alipozungumza na waandishi wa habari.
Garlus alitaja maboresho yaliyofanyika katika bandari hiyo ni kununuliwa kwa vifaa maalumu vya kubebea mizigo yaani ‘folklift’ 98 na mitambo mikubwa miwili na ya kisasa ya kushushia makasha yaani ‘SSG’.
“Vitendea kazi hivi vimefanya sasa tuwe na mitambo yenye uwezo wa kubeba mzigo wa hadi tani 200 kwa wakati mmoja na kuifanya bandari yetu ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa na yenye uwezo zaidi,” alisema.
Alisema bandari hiyo imekuwa ikihudumia kwa haraka, nafuu na ufanisi zaidi shehena ya mizigo mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa miradi hiyo ya kimkakati hapa nchini.
Akitaja vifaa vilivyopokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati, Garlus alisema hivi karibuni vichwa vitatu vya treni ya Kisasa ya mwendokasi vimepokelewa kwa ajili ya mradi wa SGR.
Vingine vilivyopokelewa, alisema ni tani 7,000 za reli ya kisasa kwa ajili ya ujenzi wa loti ya tano na mabehewa 27 ya abiria.
Mradi wa SGR unatarajiwa kuwa kiungo cha usafirishaji wa mizigo kutoka maeneo mbalimbali nchini kupeleka bandarini kwa ajili ya kusafirishwa nje ya nchi.
Hata hivyo, Desemba 31, mwaka jana Rais Samia Suluhu Hassan aliagiza kuanza kufanya kazi kwa mradi huo itakapofika Julai mwaka huu kwa kipande cha Dar es Salaam hadi Dodoma.
Kwa sasa Serikali inaendelea na ujenzi wa kipande cha sita cha mradi huo kutoka Tabora hadi Kigoma chini ya mkandarasi CCECC kutoka China.
Mbali na vifaa vya mradi wa SGR, Garlus alisema vifaa vingine vilivyipokelewa ni kwa ajili ya mradi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Mwalimu Nyerere (JNHPP).
Vifaa vilivyopokelewa, alisema ni mitambo mikubwa saba, kila mmoja ukiwa na wastani wa tani 50.
JNHPP ndiyo mradi unaotarajiwa kuwa suluhisho la changamoto ya umeme nchini. Utakapokamilika unatarajiwa kuzalisha megawati 2,115 za nishati hiyo na hadi Desemba mwaka jana ujenzi wake ulifikia asilimia 94.78.
“Hivi karibuni Bandari ya Dar es Salaam imehudumia takribani tani 17,000 za mabomba makubwa kwa ajili ya mradi wa Bomba la Mafuta la Hoima, amesema Garlus na kuongeza kwamba kuna meli nyingine 16 zinakuja na shehena ya mabomba kama hayo,” alisema.
Kadhalika, alisema uwepo wa bandari hiyo katika eneo zuri la kijografia, ufanisi na ujuzi wa watendaji wake, umechangia kupunguza gharama za ujenzi wa miradi hiyo.
Awali akipokea vifaa kwa ajili ya maboresho ya bandari hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa alisema vitasaidia kuongeza ufanisi na uwezo wa bandari.
“Vifaa hivi takribani 98 tumevipokea kwa awamu mbili na vitasambazwa katika vituo vyetu zote, lengo letu haswa ikiwa ni kuziwezesha Bandari zetu kuwa na uwezo zaidi,” alisema.
Alisema bandari za Tanzania kwa sasa zinaendeshwa katika hali ya ushindani kama zilivyo bandari nyingine duniani.
Mbossa alisema mazingira hayo yanachagizwa na mabadiliko ya ukuaji wa sekta ya usafirishaji majini, teknolojia na uchumi.
“TPA kama Taasisi iliyokasimishwa jukumu la umiliki, uendeshaji, uendelezaji na usimamizi wa Bandari nchini ina jukumu la kutoa huduma sambamba na kasi ya mabadiliko hayo," alisema. |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.