name
stringclasses
429 values
text
stringlengths
0
767k
Baada ya kukamilisha ripoti ya mapendekezo ya mageuzi ya mifumo na taasisi za haki jinai, tume iliyo
Baada ya kukamilisha ripoti ya mapendekezo ya mageuzi ya mifumo na taasisi za haki jinai, tume iliyoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuifanya kazi hiyo, imebadilishiwa jukumu na sasa inasimamia utekelezwaji wake. Tume hiyo iliyokuwa na wajumbe tisa iliundwa Januari 31, mwaka huu ikipewa jukumu la kupendekeza mageuzi ya utendaji wa taasisi 18 za haki jinai na iliikabidhi ripoti ya mapendekezo hayo Julai mwaka huu. Kutungwa kwa sheria ya haki jinai, mageuzi ya utendaji wa jeshi la polisi, magereza na mahakama ni machache kati ya mapendekezo zaidi ya 300 yaliyopendekezwa katika ripoti hiyo. Mzizi wa kuundwa kwa tume hiyo, ni kile kilichowahi kuelezwa na Rais Samia, kuna michezo michafu inayoendelea katika taasisi za haki jinai nchini. Hata hivyo, kulikuwepo na wasiwasi juu ya mapendekezo ya tume hiyo kutekelezwa, kutokana na rejea ya kuswekwa makabatini kwa ripoti za tume na kamati mbalimbali zilizowahi kuundwa, lakini kwenye hii kuna dalili njema. Dalili njema hizo zinatokana na hatua ya Rais Samia kuibadilishia jukumu tume hiyo kutoka kutoa mapendekezo hayo na sasa kusimamia utekelezwaji wake. Hayo yalielezwa jijini Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Othman Chande alipohutubia mabalozi na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, katika hafla ya kuwasilisha ripoti hiyo kwa viongozi hao wa kidiplomasia. Baada ya kukabidhi ripoti hiyo, Jaji Chande alisema Rais Samia amefanya mambo mawili ambayo ni kuiteuwa tena na kuifanya kuwa kamati ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa mapendekezo iliyoyatoa na kuiongezea wajumbe wawili. Wajumbe walioongezwa, kulingana na Jaji Chande ni Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba na Waziri Ofisi ya Rais, asiye na Wizara maalum, George Mkuchika. “Hawa wamekuja kuongeza nguvu katika ile timu ya wajumbe tisa tuliyokuwa nayo tangu awali na kwa uzoefu wao wa mambo mbalimbali watasaidia kufanikisha kazi iliyopo,” alisema. Kuhusu mabadiliko ya jukumu, alieleza kamati hiyo kwa sasa inasaidia kila taasisi kati ya zile 18 ilizopendekeza zifanyiwe mageuzi, ziandae mpango kazi na mikakati ya kutekeleza mapendekezo yaliyopo katika ripoti hiyo. Kwa mujibu wa Jaji Chande, utekelezwaji wa mapendekezo hayo unalenga kuzifanya taasisi za haki jinai ziwe na uwezo wa kubaini na kudhibiti uhalifu kabla haujatokea, badala ya kusubiri utokee ndipo zipambane nao kama ilivyo sasa. "Tunachotaka ni kuwa na taasisi za haki jinai zitakazoweza kudhibiti uhalifu kabla haujatokea, kuliko kusubiri utokee ndiyo udhibiti," alisema. Hata hivyo, Jaji Chande alisema kwa sasa kila taasisi ipendekeze kipaumbele cha mapendekezo na tayari hilo limeshaanza kufanyika tangu wiki nne zilizopita. Lakini, alieleza tayari baadhi ya mapendekezo yameshaanza kufanyika kazi, likiwemo lililotaka kuwepo ofisi za mashtaka katika kila Wilaya. "Hivi karibuni Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) alieleza kwamba ameanzisha ofisi za mashtaka katika Wilaya 50, hii tunaepuka ile ya kuwafanya Polisi kuwa na kazi ya kuchunguza, anapeleleza na anashtaki," alisema. Warioba, Mkuchika Warioba aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, amewahi kuziongoza tume mbalimbali ikiwemo ile iliyoundwa na Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ya Serikali Rushwa. Tume nyingine, iliyowahi kuongozwa na Mtaalamu huyo wa sheria ni ile iliyoundwa na Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete mwaka 2014 ya kurekebisha Katiba. Kwa upande wa Mkuchika, ndiye mwanasiasa anayetajwa kuwahi kuhudumu karibu katika Serikali zote nchini, tangu awamu ya kwanza. Katika kipindi hicho chote, Mkuchika ameshika nafasi mbalimbali za kisiasa ikiwemo ubunge, uwaziri na Mkuu wa Mikoa mbalimbali. Miongoni mwa Wizara alizowahi kuziongoza no Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), lakini sasa ni Waziri katika Ofisi ya Rais, asiye na Wizara Maalum. Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Balozi Ombeni Sefue alisema kinachofanywa sasa ni kumsaidia Rais kutengeneza njia za utekelezaji wa mapendekezo hayo. "Kwa sasa tunahusisha taasisi mbalimbali kupokea ushauri wao juu ya utekelezaji na hii ni wiki ya tatu tunafanya," alisema. Alieleza hatua hiyo itawezesha kujua kipi kinapaswa kutekelezwa kwa muda mfupi, wa kati na mrefu kisha itajulikana nani atafanya nini. Katika shughuli hizo, alisema kikao na mabalozi na wakuu wa mashirika ya kimataifa kitafanyika kupokea mapendekezo yao. "Naamini kila nchi ina njia zake ilizokuja nazo kufanya maboresho ya sera na sheria kuhusu mifumo ya haki jinai," alisema. Balozi Sefue ambaye ni Katibu Mkuu kiongozi Mstaafu, alieleza milango ipo wazi juu ya kuwajengea uwezo wajumbe hao kuhakikisha kunakuwa na rasilimali na msaada wowote wa kufanikisha utekelezaji wa mapendekezo. Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi wa Komoro nchini, Dk Ahamada El Badaoui alisema ripoti hiyo ni somo muhimu kwa wanaopaswa kujifunza. "Tunaahidi kushirikiana na Tanzania katika kufanikisha utekelezaji wa ripoti hii. Kitu muhimu cha kuzingatia ni nchi zetu kuwa na amani," alisema.
Hofu dhidi ya Serikali na kunyemelea uteuzi ni miongoni mwa mambo yaliyotajwa kuwa sababu ya kufifia
Hofu dhidi ya Serikali na kunyemelea uteuzi ni miongoni mwa mambo yaliyotajwa kuwa sababu ya kufifia kwa mijadala ya wasomi nchini. Kulingana na mwanazuoni Profesa Issa Shivji, Tanzania imepitia kipindi cha wingu zito la mijadala ya wasomi, jambo alilolitaja kama kikwazo cha maendeleo ya nchi. Kauli ya mwanazuoni huyo aliyebobea katika taaluma ya sheria, inashabihiana na mwenendo wa nchi katika utawala wa awamu ya tano chini ya Hayati John Magufuli, kipindi ambacho haikuwa rahisi wasomi kukusanyika kwa majadiliano. Katika kipindi hicho, ndipo Serikali ilipotangaza zuio la mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, jambo lililotajwa kuwa kikwazo cha demokrasia na mbinu ya kubana mianya ya uhuru wa kujieleza. Profesa Shivji alitoa kauli hiyo jana, wakati wa kongamano lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm) ndaki ya sayansi ya jamii (Coss) lililowakutanisha wanazuoni kutoka katika vyuo vikuu mbalimbali barani Afrika vikiwamo Makerere, Nairobi, Kabarak na Bujumbura. Aliisisitiza kauli yake hiyo akiitolea mfano Udsm, ambayo katika miaka ya 1970 hadi 1990 mijadala ya kitaaluma ndiyo iliyokuwa alama ya taasisi hiyo lakini utaratibu huo ukabadilika. “Kuna wakati ambapo kulikuwa na hofu nyingi kwenye chuo hiki kuzungumza au kujadili kwa sababu ya kuogopa kufuatiliwa. Kuna wakati wanafunzi wawili au watatu hawakuweza kukusanyika pamoja. “Ilifikia hatua mtu hawezi kumwalika mwingine kwa ajili ya kutoa mhadhara akisema ni lazima upate kibali, tukawa na jamii ya kibali. Kuandaa muadhara uwe na kibali na useme nani atakuja na atazungumza nini na kwa nini matokeo mihadhara na mijadala ilikufa,” alisema Profesa Shivji. Profesa Shivji aliyebobea pia katika Sayansi ya Siasa, alisema licha ya wakati mwingine mifumo ya nchi kuwabana watu wasizungumze, wanataaluma wanapaswa kuendelea kupaza sauti bila woga kwa kuwa ni jukumu lao. Hata hivyo, kauli yake inakuja katikati ya dhana kwamba wasomi wameacha kuzungumza kwa kile kinachodaiwa kujiweka katika mazingira rafiki ya kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali serikalini. Lakini, msomi huyo alieleza ni muhimu kuweka kipaumbele uhuru wa wanataaluma kwa kuwa wana mchango mkubwa katika utengenezaji wa sera na mipango mbalimbali katika nchi. “Nafahamu kuna wakati msukumo wa kisiasa unaweza usifurahishwe na watu kuzungumza, mara nyingine sio kwamba uhuru ulibanwa lakini wanataaluma wenyewe walijihisi wamebanwa hivyo kuhofia kujadili niwakumbushe wanataalum mpo huru kuzungumza,” alisema. Katika mjadala huo, uliolenga kuzungumzia mchango wa taasisi za elimu ya juu katika kuleta Suluhu katika jamii, Profesa Shivji alisema uhuru wa taaluma ni muhimu na si sawa kudhibiri vyuo kama idara za Serikali, akisisitiza wanataaluma wanapaswa kuwa huru kuzungumza bila hofu. Mtazamo wa kufifia kwa mijadala haukuwa kwa Profesa Shivji pekee, ulikuwepo hata kwa mkuu wa ndaki ya sayansi za jamii katika chuo hicho, Profesa Christine Noe aliyesema iliyopo haina nguvu kama iliyokuwepo miaka 40 iliyopita. Hata hivyo, alieleza kupitia kongamano hilo, wanazuoni watajitathmini na kujadiliana namna ya kuanzisha mijadala yenye tija kwa ajili ya kusaidia jamii na Serikali. “Tumeona kama ndaki tukae kujadili nini kimetokea, lini tulianza kupoteza umuhimu wa kusikilizwa, tunaweza kufanya nini ili wanataaluma na wanazuoni wa sasa wawe kama wa miaka ya nyuma. Wakati huo wanataaluma walikuwa wanashauri Serikali na walikuwa tegemezi tunataka turudi huko. “Kupitia mkutano huu tutaangalia sisi wenyewe ni namna gani tunawajibika kwa jamii ya ndani na kimataifa. Tunataka kuwajulisha jumuiya ya sasa ya wanazuoni kwamba tuna jukumu kubwa la kuhakikisha taaluma inaleta matokeo kwenye jamii,” alisema Profesa Christine. Profesa Christine naye, alikiri kuminywa kwa wanataaluma ingawa anaamini ni jukumu lao na kwamba atakayekuwa na sababu za kisayansi anaweza kushauri. “Ni kweli kuna kuminywa lakini tunaamini kwamba wanataaluma na sisi tunajukumu kwa sababu taaluma inafanyika kisayansi, ukiwa na sababu za kisayansi unaweza kushauri. Ninaamini mwanataaluma akiwa na matokeo ya kisayansi na akaitumia kushauri iwe Serikali au jamii lazima atasikilizwa,” alisema. Alitumia fursa hiyo kuwataka wanataaluma kujadili kwa kuzingatia majukumu yao na kuacha kuegemea kwenye siasa kwa kile alichoeleza wakati mwingine ndicho kinachochangia waonekane wameegea upande mmoja. Naibu Makamu Mkuu wa taaluma Udsm, Profesa Nelson Boniface alisema chuo hicho kinatoa uhuru kwa wanataaluma kuzungumza mambo yao kwa uhuru bila kuharibu wala kuvunja sheria za nchi. “Wanataaluma wanajua kwamba kuna uhuru wa kujieleza na hilo ndilo linalofanyika hapa katika chuo kikuu cha Dar es Salaam wako huru kuzungumza mawazo yao bila kuvunja sheria na kanuni za nchi,” alisema Profesa Boniface. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zito Kabwe alisema uwepo wa makongamo yanayojadili kuhusu uhuru wa kitaaluma ni muhimu sio tu kwa vyuo vikuu bali kwenye majukwaa yote. Alisema, “Majukwaa ya majadiliano ndiyo yanazalisha dhana, watalaam, wasomi na wanazuoni watabishana na kupata mambo ambayo yanaweza kuifanya jamii isongee mbele hii sio kwa Tanzania pekee bali ni dunia nzima. Majukwaa ya mijadala ndiyo yanajenga mataifa, mataifa ambayo hayajadiliani hayawezi kusogea mbele,”. Katika mkutano huo Profesa Shivji alizindua toleo la pili la kitabu chake cha Haki za Binadamu kilichochambua dhana ya haki za binadamu inavyotumika na watalawa wa dunia kwa kufunika dhambi zao na sio kuwashawishi watu kuendeleza mapambano yao ya kupata uhuru.
Mbinu zinazotumiwa na Serikali jijini Dar es Salaam kukomesha biashara ya ukahaba, zimekosolewa na w
Mbinu zinazotumiwa na Serikali jijini Dar es Salaam kukomesha biashara ya ukahaba, zimekosolewa na wadau, wakiitaka ianze kwa kuangalia mzizi wa tatizo, badala ya kuwakabili wahusika wa vitendo hivyo. Kulingana na wadau hao wa haki za binadamu na wataalamu wa sheria, ni muhimu kuzikabili sababu zilizowafanya wajihusishe na biashara hiyo na si kuwakabili wenyewe, wakisisitiza utafiti ni jambo la msingi kabla ya kuanza oparesheni hizo. Hata hivyo, ukosoaji huo wa wadau umejibiwa na Serikali ikisema, haikukurupuka kufikia uamuzi wa kufanya oparesheni ya kutokomeza madanguro na biashara hizo, bali ilianza kwa kufanya stadi tangu Machi mwaka huu. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ilipoanzia oparesheni hiyo, Saad Mtambule amesema pamoja na sababu mbalimbali zilizobainika, lakini si kigezo cha watu hao kutweza utu wao. Hayo yanajiri ikiwa ni wiki mbili tangu Serikali wilayani Kinondoni ianze oparesheni ya kutokomeza madanguro na biashara ya ukahaba katika maeneo mbalimbali. Hatua hiyo ya Wilaya ya Kinondoni iliungwa mkono na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Dar es Salaam, Albert Chalamila aliyeungana na wilaya hiyo kufanya ziara za kushtukiza katika madanguro mbalimbali na kudhibiti vitendo hivyo. Udhibiti wa biashara hizo jijini hapa, unaonekana kuwa mfupa mgumu uliowashinda viongozi wengi, kwani Chalamila si kiongozi wa kwanza kutangaza na kufanya oparesheni hizo, iliwahi kufanywa hivyo na Paul Makonda aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, lakini juhudi zake hazikuzaa matunda. Tutafiti chanzo Kuliko kutumia nguvu kuwadhibiti, ni muhimu kufanya utafiti wa kujua chanzo cha wanawake hao kujihusisha na shughuli hizo, kama anavyoeleza Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Ole Ngurumwa. Akizungumza na Mwananchi jana Ole Ngurumwa, alieleza chanzo hicho kisiangaliwe kwa wanaouza pekee, ni vema iangaliwe kwa nini wanaume pia wanakwenda kununua kwa wauzaji hao. “Tunapaswa kuangalia uwepo wao umesababishwa na nini, kabla ya kuwakamata na kuwafukuza. Ukiangalia asilimia kubwa ni wale wenye maisha magumu, walitelekezwa, wana watoto wanahitaji huduma. “Hawana njia nyingine ya kuendesha maisha yao na kuliko wakaibe wakaona wachague njia hiyo kujipatia fedha. “Kuna mambo mengi kama taifa tunapaswa tujadiliane na tujiulize kwa nini imefika hivyo na tuwaulize kwanini watu wanakwenda huko, tukifanya stadi mbalimbali tunaweza kujua namna gani ya kutatua tatizo kuliko kuongeza lingine,” alisema. Watafanya hadharani Kulingana na Ole Ngurumwa, kuvunja madanguro ni kutoa mwanya kwa biashara hiyo ifanyike kwa mtindo wa kujipanga barabarani. Mtindo huo, alisema ndiyo mbaya zaidi kwa kuwa unaathiri wengi hata wale wasiokuwa watumiaji na watoto, lakini wakiwa kwenye madanguro atakayekwenda ni yule muhitaji tu. “Wakati mwingine ni bora kuwa na maeneo kama hayo kuliko kukaa barabarani, kwa sababu sio kila mtu anahitaji. Tungedhibiti zaidi hii ya kukaa barabarani, lakini kunapokuwa na sehemu maalum inaweza kufanya hivyo vitu visifanyike hadharani na kuharibu utamaduni zaidi,” alisema. Hata hivyo, alisema zipo athari nyingine kwa binadamu iwapo madanguro hayo yatavunjwa, akifafanua zilikuwa nyumba za watu na ndiyo msingi wa kipato chao. Katika hatua nyingine, Ole Ngurumwa alisema pengine uwepo wa huduma hizo ni ahueni ya kutokea kwa majanga mengine, kama ubakaji na watoto kuingiliwa. “Kwa sababu kuna nafasi ya watu kwenda kutuliza mihemko yao ya kibaiolojia, kuna vitu vingine vipo kwenye jamii kwa ajili ya ku-balance maisha kwenye jamii,” alisema. Ingawa hakuthibitisha, lakini alisema uwepo wa biashara hizo katika maeneo ya Miji pengine ndiyo sababu hata vitendo vya ubakaji vimepungua na kwa sasa vimebaki zaidi vijijini ambako hakuna huduma hizo. Wengi wanafanya ukahaba kwa siri Kwa msingi wa ufafanuzi wa sheria ya makosa ya jinai ulioelezwa na Ole Ngurumwa, watu wengi wanafanya shughuli za ukahaba ingawa hawajaweka hadharani. Alieleza sheria hiyo inalitafsiri kosa la ukahaba kuwa tendo lolote la kujipatia fedha kwa njia yoyote ya ngono. Kwa maneno mengine kama uliwahi kufanya ngono ili upate fedha huo ni ukahaba. Lakini, alieleza ugumu wa ushahidi wa kosa hilo, kwa kuwa si rahisi kumkuta mtu anapokea fedha na ukathibitisha kwamba imetokana na tendo la ngono. “Mtu anaweza kumpa mtu fedha akasema ni zawadi, kwa dunia ya sasa ni vitu ambavyo hatupaswi kufuatilia sana. Lakini hakuna tofauti kwa sababu wapo watu wenye wenza kwa ajili ya kupata kitu, ni vile hawa wengine wameamua kuwa wa kweli wakajiweka hadharani,” alisema. Ilihitajika busara Mkurugenzi wa Uchechemuzi na Maboresho wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Fulgence Massawe alisema kulihitajika busara na hekima katika hatua dhidi ya wanaofanya biashara ya ukahaba, tofauti na inavyofanywa sasa. Alikiri biashara hiyo ni kinyume cha sheria, lakini mbinu inayotumika kuidhibiti inavunja maadili na kuwadhalilisha watuhumiwa. “Wanapokwenda wanawahoji wanachukua video zinarushwa na vyombvo vya habari ni kosa la kimaadili, kwa sababu wapo watu ambao hawajui kama kuna vitendo hivyo unapowaonyesha sio sawa,” alisema. Ni ngumu kufanikiwa Kulingana na mazingira ya kisheria, Massawe alisema ni vigumu kukabiliana na vitendo hivyo, akidokeza ndiyo sababu watuhumiwa wengi huishia kushitakiwa kwa uzururaji. Alifafanua kisheria uthibitisho wa shughuli ya ukahaba ni kumkuta mtu anajipatia fedha kwa kufanya ngono, jambo ambalo aghalabu ni vigumu kulishuhudia. “Unaweza kumkuta anafanya mapenzi na mtu, huo hautoshi kuwa ushahidi kwamba yeye ni kahaba, akikwambia yule ni mpenzi wake hana kosa, kunahitajika ushahidi zaidi, ndiyo maana ni ngumu kuendesha kesi hizi,” alisema. Kingine kinachoweka ugumu, alisema ni namna mbalimbali ambazo shughuli hiyo hufanyika, akifafanua mbali na wanaofanya kwenye madanguro, wengine hufanya kupitia mtandao na wapo wanaofanya wakiwa nyumbani. Maoni ya wateja Katika mahojiano na vyombo mbalimbali vya habari, baadhi ya wateja katika moja ya danguro jijini Dar es Salaam, alilalamikia uamuzi huo wa Serikali mkoani hapa, wakisema wanaonewa. “Sisi tufanye madhara mtaani? Sisi tunaishi nao tukiwa na Sh3,000 tunaenda nao sawa, hatutaki kesi,” alisema mmoja wa wateja hao bila kutaja jina. Mwingine alisema: “Mimi naona tunaonewa kutokana na kwamba hawa wanatusaidia, hatutaki kuharibu watoto wadogo na wake za watu, ndiyo maana hawa wanatusaidia matatizo yetu tunamaliza,” alisema. Utetezi wao dhidi ya machangudoa, unatokana na kile kilichoelezwa na baadhi yao kuwa, kwa kiasi kikubwa wanaofanya shughuli hizo ni salama dhidi ya magonjwa. “Siku zote wapimaji (wa Virusi vya Ukimwi) wanakuja huku na hawa (mangudoa) huwezi kufanya nao mapenzi bila kuvaa kondomu, kwa hiyo usalama ni uhakika, bila kondomu hakubali. “Wakiondoka hawa sisi tutafanyaje, mtoto wa kiume mwenyewe unaelewa zikipita siku kadhaa unataka upunguze,” alisema. Viongozi wa kimila Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania, Tonisiza Antonia alisema shughuli hizo si njema kwa misingi ya maadili, lakini Serikali inapaswa kutafuta mbinu stahiki za kudhibiti. Alipendekeza miongoni mwa mbinu hizo ni kuwaorodhesha majina na kuwawezesha kulingana na mahitaji ya kila mmoja, ili wawe na njia mbadala ya kujipatia fedha. “Kuvunja nyumba wanazofanyia shughuli hizo nisiliongelee sana, lakini Serikali inapaswa kuwatafutia shughuli mbadala, isiishie kuwazuia iwatafutie shughuli mbadala itakayowawezesha kupata fedha na kama wanafanya kwa hulka itajulikana,” alisema. Serikali: Hatukukurupuka Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule alisema hawakukurupuka kuchukua uamuzi huo, ni jambo lililoanza kwa stadi iliyofanyika tangu Machi mwaka huu. “Tulifanya utafiti wa kutosha juu ya mmomonyoko wa maadili ndani ya wilaya yetu na vyanzo vyake na tulijiridhisha juu ya visababishi vyake,” alisema. Pamoja na visababishi hivyo, Mtambule alisema si kigezo cha watu kutweza utu wao. Stadi iliyofanyika kwa mujibu wa Mtambule ilihusisha mazungumzo na wamiliki wa madanguro, viongozi wa dini, wadau wa haki jinai, maofisa ustawi wa jamii, makahaba na wananchi. “Mei mwaka huu nilifanya kikao na wamiliki wa madanguro na tuliyajua yote, mahali yalipo na wamiliki wake kwa hiyo hadi tunafanya oparesheni hii hatukukurupuka,” alisema. Hata hivyo, alieleza kinachofanywa sasa ni kuangalia namna ya kuwaunganisha na waliokuwa wanafanya biashara hizo na fursa mbalimbali zilizopo wilayani humo. “Kwa sasa tunafungua milango kwa wadada hawa (machangudoa) kuna fursa nyingi tunataka kuwaunganisha nazo zilizopo kwenye maeneo yetu,” alisema. Kwa upande wa wenye majengo hayo, alieleza wamewataka wayatumie kulingana na matakwa ya hati za umiliki na akibainika anayekiuka, watakwenda mahakamani kwa ajili ya kuyataifisha. Kwa mujibu wa Mtambule, wataendelea kuyapa misukosuko madanguro yote na wale wanaokaidi watachukuliwa hatua ikiwemo kutaifishiwa nyumba zao.
Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), imesema imekamilisha maandalizi ya vitabu vya kiada katika madarasa
Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), imesema imekamilisha maandalizi ya vitabu vya kiada katika madarasa yote yanayotarajiwa kuanza kutekeleza sera na mitalaa mipya ya elimu mwaka 2024. Madarasa yanayotarajiwa kuanza kutekeleza sera hiyo kwa shule za msingi ni darasa la awali, la kwanza hadi la tatu, huku upande wa Sekondari ni elimu ya amali. Taarifa hiyo ya TET inakuja ikiwa ni siku moja baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aeleze bungeni juu ya Serikali kukamilisha mapitio ya sera na mitalaa ya elimu na kwamba mwakani utekelezaji utaanza. Kauli kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya vitabu hivyo, imetolewa leo, Jumamosi Novemba 3, 2023 na Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dk Aneth Komba wakati wa kusaini mkataba wa makubaliano ya kutafsiri vitabu vya kiada na ziada vya wanafunzi wenye uziwi kati ya taasisi hiyo na Shirika la Maendeleo ya Utafsiri wa Lugha ya Alama Tanzania (TSLTDO). “Kwa mwaka 2024 tunatarajia darasa la awali, la kwanza na la tatu kwa elimu msingi wataanza kutekeleza sera na mitalaa mipya ya elimu na tayari vitabu vya kiada na ziada tumeshaandaa. “Kwa upande wa sekondari tutaanza na mkondo wa elimu ya amali na tayari vitabu vya ngazi hiyo vimeshaandikwa pia,” amesema Dk Aneth. Hata hivyo, amesema ombwe lililokuwepo ni kwenye vitabu vya wanafunzi wenye changamoto ya uziwi na kwamba baada ya mkataba huo vyote vitakamilika. “Ushirikiano huu ni mwendelezo wa nia ya Serikali kuhakikisha hakuna mtoto anayeachwa nyuma, Serikali inaendelea kuhakikisha kila mtoto anapata haki ya msingi ya elimu bora,” amesema. Hata hivyo, amesema ni muda mrefu kulikuwa na ombwe la vitabu vya wanafunzi wenye uziwi, hali iliyowawekea mazingira magumu ya kujifunza. “Kwa kuwa hatukuwa na utaalamu wa kuandaa vitabu vya lugha ya alama, tumeamua kushirikiana na TSLTDO. Tutawapatia nakala laini ya vitabu vyote vya kiada vinavyopaswa kutafsiriwa kwa lugha ya alama,” amesema. Rais wa TSLTDO, Sensor Msimbete amesema kabla ya shughuli hiyo, taasisi hiyo ilikuwa ikifanya kazi ya kutafsiri biblia kwa lugha ya alama. Ujuzi huo, amesema waliupata Kenya ilipotoa fursa kwa watu kwenda kujifunza kutafsiri biblia kwa lugha ya alama. “Mwaka 2007 tulisajili kampuni na tukaanza kutekeleza na majukumu mengine ya kutafsiri vitabu, tunatarajia hatua hii itawezesha kundi la wanafunzi wenye uziwi lifikiwe,” amesema. Mkurugenzi wa Elimu Maalum, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Dk Magreth Matonya amesema hiyo ni mara ya kwanza kwa wanafunzi wenye ulemavu huo kutafsiriwa vitabu. "Mwenye uziwi bila lugha ya alama hawezi kujifunza chochote, ukalimani huu wa vitabu unaenda kutusaidia kutatua changamoto kubwa iliyokuwepo shuleni," amesema.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemteuwa Aziza Ally kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Jamhuri ya Muung
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemteuwa Aziza Ally kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapunduzi (CCM). Aziza anateuliwa kushika wadhifa huo, ulioachwa wazi na Bahati Ndingo ambaye kwa sasa ni mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya. Bahati alijiuzulu nafasi ya ubunge wa viti maalum Agosti 17, mwaka huu ili kwenda kuwania ubunge katika jimbo hilo mkoani Mbeya. Nafasi ya ubunge katika jimbo hilo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa na wadhifa huo, Francis Mtega kufariki dunia Julai 1, mwaka huu kwa ajali ya pikipiki iliyogongana na Powertiller. Uteuzi huo umetangazwa leo, Jumamosi Novemba 3, 2023 kupitia taarifa kwa umma iliyotiwa saini na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhan Kailima. “Uteuzi huo umefanyika baada ya tume kupokea barua yenye kumbukumbu namba CEA.137/400/02a/22 ya tarehe 19, Agosti 2023 kutoka kwa Spika wa Bunge, (Dk Tulia Ackson) ikitaarifu tume juu ya uwepo wa nafasi iliyopo wazi ya ubunge wa viti maalum,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo. Kulingana na taarifa hiyo, uteuzi umefanyika kwa mujibu wa Ibara ya 78(4), ya Katiba ya Tanzania ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (6) na (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343. Hii si mara ya kwanza kwa Aziza kushika nafasi hiyo, amewahi kuwa mbunge wa viti maalum tangu 2005 hadi 2010, aliposhindwa kutetea nafasi yake katika mchakato wa ndani wa chama chake.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemteuwa Aziza Ally kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Jamhuri ya Muung
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemteuwa Aziza Ally kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapunduzi (CCM). Aziza anateuliwa kushika wadhifa huo, ulioachwa wazi na Bahati Ndingo ambaye kwa sasa ni mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya. Bahati alijiuzulu nafasi ya ubunge wa viti maalum Agosti 17, mwaka huu ili kwenda kuwania ubunge katika jimbo hilo mkoani Mbeya. Nafasi ya ubunge katika jimbo hilo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa na wadhifa huo, Francis Mtega kufariki dunia Julai 1, mwaka huu kwa ajali ya pikipiki iliyogongana na Powertiller. Uteuzi huo umetangazwa leo, Jumamosi Novemba 3, 2023 kupitia taarifa kwa umma iliyotiwa saini na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhan Kailima. “Uteuzi huo umefanyika baada ya tume kupokea barua yenye kumbukumbu namba CEA.137/400/02a/22 ya tarehe 19, Agosti 2023 kutoka kwa Spika wa Bunge, (Dk Tulia Ackson) ikitaarifu tume juu ya uwepo wa nafasi iliyopo wazi ya ubunge wa viti maalum,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo. Kulingana na taarifa hiyo, uteuzi umefanyika kwa mujibu wa Ibara ya 78(4), ya Katiba ya Tanzania ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (6) na (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343. Hii si mara ya kwanza kwa Aziza kushika nafasi hiyo, amewahi kuwa mbunge wa viti maalum tangu 2005 hadi 2010, aliposhindwa kutetea nafasi yake katika mchakato wa ndani wa chama chake.
Licha ya mapendekezo mbalimbali yanayoelekeza uchunguzi dhidi ya utaratibu wa kukiri makosa kwa hiar
Licha ya mapendekezo mbalimbali yanayoelekeza uchunguzi dhidi ya utaratibu wa kukiri makosa kwa hiari (Plea Bargaining), wahanga wa utaratibu huo wameonyesha wasiwasi wa suala hilo kutekelezwa. Wasiwasi wao unatokana na kile walichoeleza, kumekosekana utashi wa kisiasa wa kuchukua hatua za kiuchunguzi dhidi ya utaratibu wa Plea Bargaining uliokuwa unasimamiwa na aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) wakati huo, Biswalo Mganga ambaye sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu. Mapendekezo ya uchunguzi huo, yalitolewa juzi bungeni na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), iliyotaka uchunguzi huo ufanyike kwa kuzingatia masharti ya sheria na Katiba ili wahusike wachukuliwe hatua. PAC kupitia mwenyekiti wake, Japhet Hasunga ilisema: “Serikali ifanye uchunguzi wa kina na mahsusi katika suala hili kwa kuzingatia masharti ya katiba na sheria ili wahusika wachukuliwe hatua ipasavyo kwa dosari zilizojitokeza katika mchakato huu.” PAC haikuwa ya kwanza kupendekeza hilo, Ripoti ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere iliwahi kufanya hivyo pia, ikiitaka mamlaka ya uteuzi wa aliyekuwa Mwendesha Mashtaka Mkuu-DPP (bila kumtaja jina) iunde tume ya kuchunguza matumizi mabaya ya ofisi yake. “Napendekeza mamlaka za uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ziunde tume huru ya kuchunguza uwezekano wa ukiukwaji wa maadili na matumizi mabaya ya ofisi ya umma katika mchakato wa kukiri makubaliano ya kukiri kosa,” alieleza CAG katika ripoti yake. Katika uchunguzi wake, Kichere alibaini Sh6.1 bilioni zilizokusanywa kupitia utaratibu huo, ziliwekwa kimakosa kwenye akaunti tofauti na ile ya Plea bargaining. Mbali na hizo, alisema ukaguzi huo pia, umebaini jumla ya Sh1.3 bilioni zilizokusanywa ziliwekwa hazina bila kupitia katika akaunti ya Plea Bargaining. Si hivyo, alieleza hakukuwa na ushahidi kwenye kitabu cha fedha wala risiti za mapokezi ya fedha hizo. Malalamiko dhidi ya utaratibu huo, yalitolewa hata na Rais Samia Suluhu Hassan alipozindua tume ya kurekebisha mfumo wa haki jinai jijini Dodoma. Alisema: “Ofisi ya Taifa ya Mashataka kulikuwa na ngoma kubwa inachezwa, mpaka kukusanya fedha za wale wa Plea Bargaining. Fedha zile nyingine zinaonekana na nyingine hazionekani. “Uki-trace (ukifuatilia) utaambiwa kuna akaunti China, sijui zimepelekwa pesa zipi. Tukatizame haya yote kuna hasa kilichoikumba Ofisi ya taifa ya mashtaka,” alisema. Kauli za wahanga Akizungumza na Mwananchi jana, Mwanahabari, Erick Kabendera aliyewahi kukumbwa na madhila hayo, aliliambia Mwananchi, pamoja na mapendekezo ya PAC na mamlaka nyingine zilizowahi kuzungumzia hilo, kuna ishara ya kukosekana utashi wa kisiasa juu ya uamuzi huo. Inavyoonekana kulingana na Kabendera, siasa na upepo wa nchi unakwamisha uamuzi wa hatua za kiuchunguzi dhidi ya utaratibu wa Plea Bargaining. “Kuna uoga kwamba watu wanaoweza kukamatwa kwa makosa waliyoyafanya wakati jambo hilo linafanyika inaweza kuleta shida kisiasa,” alisema. Lakini, alisema kutofanyika kwa uchunguzi na hatua dhidi ya utaratibu huo, kunaendelea kuacha makovu kwa wananchi hasa wale waliowahi kuumizwa nao. “Kuna mambo matatu hapa, CAG alipendekeza, Rais aliwahi kusema hizi fedha zimefichwa China, ile tume ya kurekebisha mfumo wa haki jinai ilipendekeza uchunguzi pia, kinachokosekana ni utashi wa kisiasa,” alisema. Mbaya zaidi ni kile alichofafanua, uzoefu unaonyesha nchi zilizopitia madhila kama ya Tanzania, yasiporekebishwa kuna uwezekano wa kujirudia siku zijazo. Alionyesha kushangazwa na hatua ya baadhi ya watu walioonekana kuhusika na utaratibu huo, wanarudishwa kwenye mifumo ya Serikali na chama (CCM) kushika nafasi mbalimbali. Hata hivyo, Kabendera alisema pasi na utaratibu wa kijaji, itakuwa vigumu kwa mapungufu yaliyoonekana kuzibika. Muhanga mwingine wa mfumo huo ni Tito Magoti, aliyeeleza kukubaliana na mapendekezo ya PAC, akisisitiza suala hilo haliwahusu wahanga wa Plea Bargaining pekee. Alisema hilo linawahusu wananchi wote kwa kuwa, suala hilo haliwahusu wahanga pekee, hadi wananchi wengine linawahusu. Kwa mujibu wa Magoti ambaye pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu, iwapo suala hilo litatekelezwa litajenga taswira njema ya mahakama kwa umma na lisipotekelezwa itakuwa kinyume chake. “Ni muhimu madukuduku yaliyotokewa dhidi ya Biswalo (Mganga, DPP mstaafu) yakachunguzwa na uamuzi ufanyike,” alisema. Kwa kuwa uchunguzi wa utaratibu huo kulingana na wadau, utamhusisha Biswalo, ambaye sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu aliyeteuliwa na Rais Samia tangu Mei 11, mwaka 2021, majaji wastaafu wanaeleza taratibu za uchunguzi wa mtu mwenye hadhi hiyo. Uchunguzi dhidi ya Jaji Alipoulizwa kuhusu utaratibu wa uchunguzi dhidi ya jaji, Jaji Kiongozi mstaafu, Amir Manento alisema zipo taratibu zinazopaswa kufuatwa katika utekelezaji wa hilo. Kulingana na Jaji Manento, uchunguzi dhidi ya jaji unapaswa kufanywa na tume ya maadili ya kiongozi huyo inayoundwa na majaji wenzake. Lakini, alifafanua kamati hiyo inaundwa na majaji watatu na wawili kati yao wanapaswa kutoka katika nchi za Jumuiya ya Madola. “Mwenyekiti wa kamati hiyo anapaswa kutoka katika moja ya nchi hizo (Kenya au Uganda) na wajumbe hawapaswi kuwa miongoni mwa watu watakaokuwa na maslahi au hofu dhidi ya anayechunguzwa,” alisema. Inafanyika hivyo, ili kulinda kile alichokiita uhuru wa mahakama na kuepusha mgongano wa maslahi katika uchunguzi husika. “Mjumbe wa tume hiyo hapaswi kuwa mmoja wa wale ambao pengine atakuwa na hofu ya kupoteza ajira yake kwa kumchunguza jaji husika au vinginevyo,” alieleza Jaji Manento. Hata hivyo, alieleza mkuu wa nchi hawezi kuunda tume hiyo kwa kuwa, hata ajira ya jaji haitokani naye moja kwa moja. Kwa upande wa Jaji kiongozi mstaafu, Fakih Jindu alisema taratibu hizo zitafuatwa iwapo tuhuma za jaji husika hazihusishi jinai. Kama zinahusisha jinai, alifafanua jaji husika atachunguzwa kwa utaratibu kama ambavyo wananchi wengine huchunguzwa, isipokuwa mamlaka za mahakama lazima zijulishwe. Kulingana na Jaji Jindu, iwapo tuhuma zinahitaji kumuondoa kiongozi huyo kwenye nafasi yake, lazima kuundwe kamati itakayohusisha majaji kutoka nje ya Tanzania. “Kama anataka kuondolewa kwenye nafasi yake lazima kuwe na kamati yenye majaji kutoka ndani ya nje ya nchi na hao ndiyo watachunguza tuhuma husika kisha itaonekana nini cha kufanya,” alisema. Kinyume na mitazamo ya majaji hao, Magoti alisema utaratibu wa nidhamu ya majaji umebainishwa katika Ibara ya 110 (A) ya Katiba ya Tanzania. Kulingana na ibara hiyo, Magoti alisema Rais atashauriana na Jaji Mkuu baada ya kupokea dokezo la malalamiko, kisha atamsimamisha kazi jaji husika na kuunda baraza maalum la kumchunguza litakalopendekeza hatua dhidi yake. “Kwa mazingira yetu na muktadha huu dokezi linaweza kujumuisha ripoti ya CAG na hata kauli nyake mwenye Rais Samia kuhusu Plea Bargaining. Lakini malalamiko ya wananchi, vyama vya siasa na vyombo vya habari vimewahi kuandika,” alisema.
Imechukua zaidi ya karne tangu mabaki ya miili ya Watanzania yahifadhiwe katika makumbusho mbalimbal
Imechukua zaidi ya karne tangu mabaki ya miili ya Watanzania yahifadhiwe katika makumbusho mbalimbali nchini Ujerumani na sasa uamuzi wa kuyarejesha umefikia hatua nzuri. Baadhi ya mabaki hayo ni yake ya miili ya machifu na viongozi mbalimbali waliokuwa vinara katika vita vya Tanganyika dhidi ya Ujerumani (Maji Maji), mwaka 1905/07. Hatua ya kurejeshwa kwa mabaki hayo, ilidokezwa jana na Rais Samia Suluhu Hassan, alipozungumza na waandishi wa habari baada mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier yaliyofanyika Ikulu ya Dar es Salaam. Alisema miongoni mwa majadiliano aliyoyafanya na Rais huyo ni kuangalia uwezekano wa kurejesha mabaki ya miili ya Watanzania iliyopo nchini humo. Mazungumzo hayo ni sehemu ya ratiba ya Rais Steinmeier aliyewasili nchini jana kwa ziara ya kikazi ya siku tatu. Alisema, "najua kuna familia ambazo zinasubiri mabaki ya miili ya ndugu zao ambayo yapo kule katika makumbusho mbalimbali za Ujerumani, yote hayo tunakwenda kuyazungumza na kuona vipi tutakwenda nayo vizuri." Katika hotuba yake mbele ya waandishi wa Habari, Rais Steinmeier naye alieleza mpango huo, akidokeza unatarajia kufanyika kwa siku zijazo. Alisema hilo litaambatana na kupeleka Ujerumani taarifa za hali za wahanga wa vita vya majimaji anaotarajia kukutana nao kesho. Agizo la kurejeshwa kwa mabaki ya Watanzania yaliyopo Ujerumani, aliwahi kulitoa Januari 21, 2022 alipohutubia tamasha la machifu nchini. Hata hivyo, Januari mwaka huu, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohammed Mchengerwa alikutana na Balozi wa nchi hiyo, Rejine Hess kwa mazungumzo kuhusu hatua hiyo. Ushirikiano Katika hatua nyingine, wawili hao wamekubaliana kukuza ushirikiano baina ya mataifa hayo mawili kwa manufaa ya wananchi wao. Rais Samia alimhakikishia Rais Steinmeir kuwa Tanzania ipo tayari kuwa mwenyeji wa mazungumzo yajayo ya ushirikiano wa maendeleo yatakayofanyika mwaka ujao. Kuhusu biashara na uwekezaji, Rais Samia na mgeni wake walisitiza umuhimu wa mchango wa biashara na uwekezaji katika kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. “Tumekuwa na miradi isiyopungua 100 ya Ujerumani katika ngazi mbalimbali iliyowekezwa, lakini tumekuwa tukifanya biashara. Lakini baadaye kutakuwa na kongamano la wafanyabiashara wa Tanzania na Ujerumani litakalojadili fursa za uwekezaji,” alisema Rais Samia. Mauzo ya biashara ya kutoka Tanzania kwenda Ujerumani kwa mwaka ni Dola za Marekani 42.04 milioni ambapo ni bidhaa za kahawa, tumbaku, pamba na asali, samaki, nta na madini. Rais Samia alisema Tanzania imekuwa ikipata utalii kutoka Ujerumani na kwamba upo uwezekano wa kuongeza zaidi iwapo watajitangaza vema. Rais Samia alisema mashirika ya Ujerumani yamekuwa yakisaidia uhifadhi wa mbuga za Selous na Serengeti. Ujerumani ni miongoni wa nchi sita zinazoongoza kwa watalii nchini na mwaka huu Tanzania imepokea watalii 67,718 kutoka taifa hilo. “Ziara hii inathibitisha dhamira ya Serikali hizi mbili ya kuimarisha na kukuza ushirikiano na urafiki wetu kwa lengo la kuwanufaisha wananchi,” amesema Rais Samia. Akizungumza katika mkutano huo, Rais Dk Steinmeier alisema Ujerumani itaendelea kuwa mshirika wa Tanzania katika maeneo mbalimbali. Katika ziara hiyo, leo Dk Steinmeier atawatembelea waathirika wa vita vya maji maji mkoani Ruvuma.Vita hiyo iliongozwa na Kinjekitile Ngwale aliyenyongwa mwaka 1905. Vita vya maji maji vilitokea kati ya 1905 hadi 1907. Inakadiriwa kuwa kati ya watu 180,000 hadi 300,000 walifariki dunia wakati wa vita hivyo huku sababu nyinginezo kama njaa na magonjwa zikitajwa kuchangia vifo hivyo.
Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier, anatarajiwa kufanya ziara ya ki
Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier, anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini kuanzia kesho hadi Novemba 1, 2023. Hayo yameelezwa leo, Oktoba 29, 2023 kupitia taarifa ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kulingana na taarifa hiyo, ziara hiyo mbali na kudumisha uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa maendeleo baina ya Tanzania na Ujerumani, pia imelenga kukuza na kuimarisha misingi ya biashara na uwekezaji. Imeeleza ujumbe wa rais huyo utakaojumuisha viongozi wa Serikali ya nchi hiyo na wawekezaji wa kampuni 12, utawasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam kesho. “Ugeni huo utapokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,” amesema. Baada ya kuwasilia, taarifa hiyo inaeleza, Rais Steinmeier atafanya mazungumzo mwenyeji wake, Rais Samia Suluhu Hassan Oktoba 31, mwaka huu. “Baada ya mazungumzo hayo, viongozi hao watapata fursa ya kuongea na Waandishi wa Habari kuelezea kuhusu masuala muhimu yaliyofikiwa wakati wa mazungumzo yao,” amesema. Imeeleza wawili hao watashiriki Jukwaa la Biashara, litakalohusisha wafanyabiashara na wawekezaji wa nchi hizo mbili, lililoandaliwa na Ubalozi wa Ujerumani kwa ushirikiano na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Mazungumzo na vijana wa Tanzania, kutembelea kiwanda cha Twiga Cement na makumbusho ya vita vya majimaji mkoani Songea ni miongoni mwa shughuli zinazotrajiwa kufanywa na ugeni huo. Uhusiano wa nchi hizo Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na TIC, Tanzania imekuwa ikiuzia Ujerumani bidhaa zenye thamani ya wastani wa Dola za Marekani milioni 42.04 kwa mwaka. Bidhaa kuu ambazo Tanzania inaiuzia Ujerumani ni Kahawa, Tumbaku, Pamba, Asali, Samaki, Nta na vito vya thamani. Kadhalika, Tanzania inaagiza bidhaa kutoka Ujerumani zenye wastani wa Dola za Kimarekani milioni 237.43 kwa mwaka na bidhaa kuu ni Dawa, Vifaa Tiba, Mafuta (manukato, vipodozi) Magari, Vifaa na Mashine za Umeme. Kwa upande wa uwekezaji, Ujerumani ni miongoni mwa nchi kumi zinazoongoza kwa uwekezaji nchini. Kwa mujibu wa TIC hadi Agosti mwaka huu, miradi 178 ya Ujerumani yenye thamani ya Dola za Marekani 408.11 milioni ilisajiliwa na kutoa fursa za ajira 16,121. Kwa upande wa Zanzibar, Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) imesajili miradi 15 yenye thamani ya Dola za Marekani 300 milioni iliyozalisha ajira 905.
Ili kuongeza upatikanaji wa taarifa za Serikali kwa wananchi, Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Mati
Ili kuongeza upatikanaji wa taarifa za Serikali kwa wananchi, Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema ofisi yake inatarajia kwenda katika Mikoa mbalimbali nchini kuwapa nafasi Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa halmashauri waeleze kilichofanywa na Serikali katika maeneo yao. Amesema utaratibu huo unatarajiwa kuzinduliwa Novemba 1, mwaka huu mkoani Dodoma chini ya uratibu wa Idara ya Habari Maelezo. Matinyi alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza katika mkutano wake na wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari. “Tutafika katika Mkoa, atakuja na wakuu wake wa Wilaya lakini tunataka tuwape nafasi wakurugenzi wa halmashauri kwa sababu tunataka kusikia habari za utekelezaji na katika muundo wetu fedha zinapelekwa kwenye halmashauri,” alisema. Dhamira ya uamuzi huo, Matinyi alisema ni kuwajuza watanzania juu ya kinachofanywa na Serikali katika maeneo mbalimbali nchini. “Programu hii baada ya Dodoma tutakwenda Morogoro, kisha Pwani na Dar es Salaam, ili kufanikisha tumetanguliwa timu ya waandishi wa habari kwenye maeneo hayo wamewahoji wananchi na wakurugenzi na zitaonyeshwa makala,” alisema. Alieleza makala hizo zitarushwa katika vyombo mbalimbali vya habari na kwamba baada ya Mikoa hiyo itakayofuata ni Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga. "Serikali inafanya mambo mengi lakini wananchi hawana habari, nikiwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, nilikumbana na jambo ambalo lilinifanya nione kuna umuhimu hili jambo liwepo," alisema. Hata hivyo, alisisitiza katika kipindi cha uongozi wake atahakikisha kunakuwepo na ushirikiano kati ya waandishi wa habari na viongozi wa Serikali. Msisitizo huo wa Matinyi ulitokana na kauli ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile aliyesema pamoja na ushirikiano mkubwa kutoka kwa viongozi wa juu, lakini wapo watendaji ndani ya Serikali ni wagumu kutoa taarifa. Kuhusu hoja hiyo, Matinyi alijibu angalau viongozi wa kisiasa wana uzoefu wa kuzungumza na vyombo vya habari, lakini alikiri uwepo ugumu kwa baadhi ya watendaji. Alieleza ugumu huo aghalabu husababishwa na kumbukumbu za kuwahi kunukuliwa vibaya na vyombo vya habari hivyo, wanaishia kuhofu kuzungumza na wanahabari. “Unakuta aliwahi kuhojiwa akatoa taarifa mwandishi wa habari akamnukuu vibaya leo anaogopa kuongeza kwa sababu hiyo, wakati ni kosa la kibinadamu, hili tutaweka sawa,” alisema. Kibano kwa Makanjanja Aliihusianisha hoja yake hiyo na mchakato wa utekelezwaji wa sheria na sera za taaluma ya habari nchini, akisema kanuni ya sheria ya huduma za habari ya mwaka 2016 inatarajiwa kufanyika marekebisho. Katika marekebisho hayo, Matinyi alisema pamoja na sheria kumtaka Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, lakini ametaka wadau wa habari wahusihwe. “Tayari utaratibu umepangwa watapata barua na rasimu ya kanuni ili wazipitie watoe maoni yao kufikia Novemba 10 wayawasilishe habari maelezo na Novemba 18 au 19 kutegemeana na ratiba ya waziri atakutana na wadau,” alisema. Katika hilo, alieleza sheria hiyo inataka kuundwa kwa bodi ya ithibati ya wanahabari ambayo kisheria inahitaji majina ya waandishi wa habari watakaokuwa sehemu ya wajumbe. “Tuliomba vyombo vya habari vituletee majina na tunashukuru vyombo vya habari vimetuletea majina, mchakato utakaofanyika litateuliwa jina kulingana na mapendekezo na nadhani kufikia Desemba kama mambo yatakwenda sawa sawa tutakuwa tumeipata bodi hiyo,” alisema. Kuundwa kwa bodi hiyo, alisema kutafuatiwa na kuundwa kwa Baraza Huru la Vyombo vya Habari na kisha utaundwa mfuko wa mafunzo ya waandishi wa habari. “Muda sasa umefika vya kutosha tunakwenda kukamilisha vile vyote ambavyo sheria inavitaka,” alisema. Katika mkutano huo, Matinyi alitangaza ziara ya waandishi wa habari katika bandari ya Dar es Salaam, ili kujua shughuli na taarifa nyingine mbalimbali kuhusu eneo hilo. Alieleza uamuzi huo unatokana na ukweli kwamba, idadi kubwa ya watanzania wakiwemo wanahabari hawaijui bandari hiyo kwa kina. Akijibu swali la mmoja wa wanahabari kuhusu usiri wa hafla ya kusainiwa kwa mikataba mitatu ya mradi wa bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia DP World, alisema hakukuwa na usiri. Alieleza kila kitu kilifanyika hadharani na hata hotuba zilieleza mambo mengi na zaidi, matukio yote yalirushwa mubashara kupitia vyombo vya habari. Awali, akizungumza katika mkutano huo. Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile alitaja baadhi ya mambo waliyozungumza ni umuhimu wa vyombo vya habari, ushirikiano na uendelevu. “Lakini jingine ni mazungumzo kuhusu misingi ya taaluma ya habari bila kuathiri utamaduni au kupotosha,” alisema Balile.
Tanzania imetupa karata yake kugombea nafasi ya Urais wa Bunge la Dunia (IPU) katika uchaguzi unaota
Tanzania imetupa karata yake kugombea nafasi ya Urais wa Bunge la Dunia (IPU) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, huku Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson akiteuliwa kuipeperusha bendera ya nchi kuwani nafasi hiyo. Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kushiriki kinyang’anyiro hicho, kadhalika iwapo itashinda itakuwa nchi ya kwanza Afrika kuukwaa wadhifa huo. Si hivyo tu, iwapo Dk Tulia ataukwaa wadhifa huo, atakuwa mwanamke wa kwanza kuliongoza Bunge hilo, lenye nchi wanachama 179 na wabunge 705 wanaoziwakilisha nchi zao. Hata hivyo, kushika wadhifa huo si sifa tu kwa Tanzania, bali kutaitangaza nchi kimataifa. Hayo yalielezwa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax baada ya kikao na mabalozi wa nchi mbalimbali kuhusu Tanzania kuwania nafasi hiyo. “Katiba jitihada zetu za kumnadi mgombea tumeona lazima tukutane na majirani zetu na ombiletu limepoelekewa vizuri na wenzetu ambao wanafahamu uwezo wake,” alisema. Kwa sababu inayowania nafasi hiyo ni Tanzania, Dk Tax alisema ni jukumu la kila mmoja kwenye nafasi yake kumnadi Dk Tulia katika wadhifa huo anayowania. Maboresho ya kuhakikisha changamoto za dunia zinakoma, kuimarisha amani, kuhamasisha wanawake kuwa sehemu ya maendeleo na uongozi ni miongoni mwa vipaumbele vya Dk Tulia kwa mujibu wa Dk Tax. “Anatarajia kuboresha uhusiano ndani ya Umoja wa Mataifa (UN) kwa sababu wanachama wa IPU ni wanachama wa UN,” alisema. Kwa mujibu wa Waziri huyo, nafasi hiyo itaitangaza Tanzania kimataifa na kupata nafasi ya kuyasimamia masuala yenye maslahi ya kidunia. Uteuzi wa Dk Tulia kuwania nafasi hiyo, umetokana na kile kilichoelezwa na Dk Tax kuwa anastahili kutokana na uwezo na uzoefu alionao kwenye uongozi. Bunge hilo lililoanzishwa mwaka 1889 kama kundi dogo la wabunge waliopigania amani, kwa sasa Duarte Pacheco kutoka Ureno ndiye anayeliongoza kwa nafasi ya urais. Akizungumzia hilo, mwakilishi wa Tanzania katika IPU, Elibariki Kingu alisema nafasi hiyo ni muhimu kwa nchi kwani nafasi hiyo inakuwa na wadhifa kubwa kwenye mashirika ya kimataifa. “Tukiweka ajenda hii mbele kwa maslahi ya nchi, tutaitangaza nchi na kuinua diplomasia na kutoa nafasi ya kuonyesha Tanzania inathamini malengo ya dunia ya kumpa nafasi ya uongozi mwanamke,” alisema. Kulingana na utaratibu wa IPU, Kingu alisema nafasi hiyo inaongozwa kwa miaka mitatu, kisha anafuata mwingine. Kingu ambaye pia ni mbunge wa Singida Magharibi, alisema usikivu, uwezo, malengo makubwa ni miongoni mwa sifa alizonazo Dk Tulia. Dk Tulia ni nani Licha ya kubobea katika taaluma ya sheria akiwa na Shahada ya Uzamivu ya fani hiyo, Dk Tulia amewahi kuwa Nibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mwaka 2015. Wadhifa huo aliukwaa akitokea kuwa Mhadhiri Mwandamizi katika Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 2014 hadi 2015. Mwaka huo pia, aliteuliwa na Hayati John Magufuli rais wa wakati huo, kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye kuchaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge hilo. Mwaka 2021, baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Spika wa bunge hilo, Job Ndugai mbunge huyo wa Mbeya Mjini, alichaguliwa kuwa Spika wa bunge nafasi aliyonayo hadi sasa.
Rais Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali inatarajia kuongeza siku za usafiri bila viza kwa wananch
Rais Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali inatarajia kuongeza siku za usafiri bila viza kwa wananchi wa Zambia wanaoingia nchini kutoka siku 90 za sasa hadi 190. Utekelezaji wa hilo, utatoa uhuru wa usafiri kwa W azambia kuingia nchini na kukaa kwa siku 190 bila kulazimika kununua viza. Rais Samia ametangaza mpango huo jana, alipolihutubia bunge la Zambia, wakati akihitimisha ziara yake ya siku tatu nchini humo. Katika hotuba yake hiyo, alisema uamuzi huo tarajiwa unalenga kurahisisha usafiri na usafirishaji wa watu kati ya nchi hizo mbili na hatimaye kufungua milango ya biashara. “Ninayo furaha ya kulitaarifu bunge hili, Serikali ya Tanzania inajiandaa kuwezesha usafiri wa watu bila visa kwa kuongeza muda wa watu kuingia nchini bila viza kutoka siku 90 hadi 190,” alisema. Katika hilo, alieleza Tanzania ipo tayari kusaidia ujenzi wa mpaka wa Zombe ili kurahisisha usafiri wa watu na usafirishaji wa bidhaa kati ya mataifa hayo. Kulingana na Rais Samia, hatua hiyo inalenga kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo na watu wake kwa ujumla. Hata hivyo, alisema ni muhimu wabunge wa mataifa hayo ambao ndiyo wawakilishi wa wananchi, kuhakikisha wanapitisha mipango na bajeti zinazowasilishwa na Serikali kwa manufaa ya umma. “Iwapo wabunge hawatashawishika au wakiamua kufanya siasa dhidi ya mipango hii, wataathiri maendeleo tuliyofikia, watanzania na wazambia,” alisema. Alieleza mrejesho unaopatikana kutoka kwa watu mbalimbali ni kwamba mifumo ya kisheria baina ya nchi hizo itakuwa rafiki kwa biashara iwapo mataifa hayo hayataingiza siasa kwenye mipango yao. Kwa sababu hiyo, alisema Serikali zinapowasilisha mapendekezo ya kuondoa vikwazo vya kikodi na ushuru, mabunge yanapaswa kujua msaada wao unahitajika. Alieleza mipango ijayo ya Serikali ni kuhakikisha inajengwa miradi mipya ya miundombinu kwa ushirikiano. Kwa mujibu wa Rais Samia, biashara ya Tanzania na Zambia itakuwa kutokana na juhudi mbalimbali ikiwemo ya kuboreshwa kwa bandari ya Dar es Salaam. Hata hivyo, Rais Samia alisema uhusiano uliopo kati ya mataifa hayo ni historia iliyobebwa na waasisi wake, Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania na Kenneth Kaunda wa Zambia. “Kuna muendelezo wa uhusiano kati ya nchi hizi mbili kwa kuwa yapo mambo yaliyobaki kama alama, likiwemo bomba la mafuta la Tazama na reli ya Tazara,” alisema. Hata hivyo, alieleza Serikali hizo mbili, zinafanya juhuzi kupunguza changamoto mbalimbali zinazoikumba reli ya Tazara ili kurahisisha usafirishaji. Katika hotuba yake hiyo, alisisitiza kuendelea kushirikiana na taifa hilo na kwamba ziara aliyoifanya itaimarisha uhusiano kati ya nchi hizo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo amewataka wabunge wa viti maa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo amewataka wabunge wa viti maalum wasiishie kujipendekeza kwa wajumbe pekee, badala yake wawe wanafanya vikao vya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kwani ndiyo msingi wa nafasi walizopewa. Kauli ya Jokate, inatokana na kile alichodokeza, kumekuwepo na tabia ya baadhi ya wabunge wa viti maalum wanaotokana na jumuiya hiyo, kutofanya mikutano ya hadhara na wananchi, wanaishia kujipendekeza kwa wajumbe. Wajumbe wanaozungumziwa na Jokate ni wale washiriki halali wa kikao cha baraza kuu la UWT, ambao aghalabu ni Wenyeviti, Makatibu na Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za UWT ngazi ya Taifa, Mikoa, Wilaya na Kata. Jokate alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na vyombo vya habari kutoa taarifa ya ziara ya kamati ya Utekelezaji ya UWT iliyofanyika katika Mikoa 10 nchini Julai hadi Oktoba mwaka huu. Kulingana na Jokate, tabia ya wabunge hao kutofanya mikutano hiyo ya hadhara, imebainika baada ya ziara ya kamati ya utekelezaji ya jumuiya hiyo taifa, iliyomhusisha Mwenyekiti wa UWT, Mary Chatanda. Aliwataka wabunge hao kuhakikisha wanafanya mikutano hiyo ili kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kwa kuwa ndiyo kazi ya msingi ya kuteuliwa kwao. "Ukipewa dhamana unapewa na CCM, lakini sisi UWT tumepewa nafasi katika kuchochea uwakilishi wa wanawake kwenye nafasi mbalimbali za maamuzi, ni vema tukaondokana na ile kasumba kwamba tunajihusisha na wajumbe pekee. “Kila siku mnakwenda kwa wajumbe mnagawa khanga na vitu mbalimbali, lakini hamfanyi mikutano ya hadhara kusikiliza na kutatua kero za wananchi, sasa hii hatuitaki,” alisema. Na katika kusisitiza utekelezwaji wa hilo, Jokate alisema ameandika barua kwenda kwa viongozi wa ngazi mbalimbali, akiamini zitafanyiwa kazi. Akitoa muhtasari wa ziara hiyo, katibu mkuu huyo alisema jumla ya wanachama 514,032 wamejiunga na CCM, mikutano 733 ya hadhara imefanyika katika Kata 750 na Wilaya 62, huku miradi 1,284 ikikaguliwa. Msimamo wa UWT Alitoa msimamo wa jumuiya hiyo, utakapofika wakati CCM inahitajika kutaja mgombea wake wa urais, UWT itakwenda kumchukulia fomu. "Tumesema wakati ukifika na CCM kitakapohitaji mgombea wa urais, sisi UWT tutakwenda kumchukulia fomu Rais Samua kwa sababu tumeona amefanya kazi kubwa ya kuwaingiza wanawake kwenye nafasi za uongozi," alisema. Hata hivyo, aliwataka wanawake kujitokeza kwa wingi kuwania uongozi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwakani. "Tunataka wanawake sasa hivi tuingie ulingoni, tusiendelee kuwa wasindikizaji na niwahakikishie UWT haitakuwa kikwazo cha wanawake wanaotaka kugombea, sana sana tutakuwa daraja la kuwasemea," alisema. Katika hatua nyingine, Jokate alitangaza vikao vikuu vya jumuiya hiyo vinavyotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar, kikiwemo cha sekretarieti, kamati ya utekelezaji na Baraza Kuu la UWT. Alieleza tayari timu ya Mwenyekiti na Kamati ya Utekelezaji kuanzia Oktoba 25, umeshaanza kutembelea Mikoa mbalimbali ndani ya visiwa hivyo na miradi imetembelewa. Lakini, alisema mwisho wa vikao hivyo, jumuiya hiyo itafanya tukio kubwa la kusherehekea miaka mitatu ya uongozi wa Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi, huku kauli mbiu ikiwa ni 'miaka mitatu ya mafanikio neema ziendelee'. "Tunaendelea kuwapa moyo viongozi wetu Wakuu, kazi wanayofanya ni kubwa, ya kutumika hakuna anayeweza kuwalipa zaidi ya Mungu," alisema.
Wakati wananchi wakitaka kuwekwa wazi kwa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa bandari ya Dar es Sala
Wakati wananchi wakitaka kuwekwa wazi kwa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa bandari ya Dar es Salaam, Serikali imesema ni vigumu kutekeleza hilo, kwa kuwa ni kinyume na matakwa ya kisheria. Hoja ya uwazi wa mikataba hiyo iliambatana na pongezi za kuzingatiwa kwa maoni ya wananchi katika utengenezaji wa mikataba hiyo mitatu iliyotiwa saini jijini Dodoma jana. Miongoni mwa waliotaka uwazi huo ni Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima aliyesema maaskofu wanasubiri kuona maandishi. “Maaskofu wanahitaji kuusoma, kusikia tu wameona na walikuwepo watatu kushuhudia tukio na walipoitwa hawakuambiwa kuna nini,” alisema. Mwingine aliyeibua hoja hiyo ni Mkurugenzi wa Jukwaa la Katiba (Jukata), Bob Wangwe aliyesema ili kujiridhisha na kauli kwamba imezingatia maoni ya wananchi ni vema mikataba hiyo iwekwe wazi. Lakini, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa alisema mikataba ya kibiashara kwa mujibu wa sheria haiwekwi hadharani. Akizungumza na Mwananchi jana, Mbossa alisema: “mkataba wa kibiashara kati ya TPA na DP World haitolewi hadharani kwa sababu kila mtu anawashindani wake.” Alieleza kipo kifungu cha sheria kinachosisitiza usiri kwa pande zote na kikikiukwa kinaweza kusababisha kuvunjwa kwa mkataba au fidia. “Ukikiuka unaweza kusababisha kuvunja mkataba au kulipa fedha tena zinaweza kuwa nyingi tu. Lakini ukiwaonyesha washindani wake wanaweza kusema mbona hawa mmewapa mambo mazuri, lakini kama kuna mtu anataka kuna njia za kufuata,” alisema Mbossa. Kauli kama hiyo ilitolewa pia na mmoja wa walioshiriki majadiliano ya mkataba huo ambaye hakutaka kutajwa jina alisema kisheria mikataba ya kibiashara haiwekwi hadharani. “Jamani ile si ni mikataba ya kibiashara na kisheria inakuwa siri, sasa wanatakaje iwekwe wazi, Tuvunje sheria?” alisema. Kwa upande wake, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Eliezer Feleshi alisema utendaji wa Serikali unasimamiwa na bunge ambalo ndilo linalowawakilisha wananchi. “Ukifika wakati kamati ya bunge husika au bunge kwa ujumla itajua. Serikali kazi zake zinasimamiwa na bunge na inafanya kazi zake kwa mujibu wa sheria,” alisema. Akilisisitiza hilo, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Harold Sungusia alisema kuwekwa wazi kwa mkataba kunatokana na makubaliano. Lakini, alieleza mara nyingi mikataba ya kibiashara haiwekwi hadharani kutokana na vifungu vya usiri vinavyotaka watu wachache ndiyo waone kilichomo. Hata hivyo, Mwanasheria huyo alisema kuwekwa wazi kwa mkataba huo kutasaidia kuongeza uwajibikaji na kudhibiti rushwa, kadhalika inatoa fursa kwa wananchi kutoa maoni yao juu ya jambo hilo kwa kuwa lina maslahi ya taifa, kama ilivyokuwa katika mkataba wa makubaliano IGA. "Kwa miaka mingi, hata wabunge wamekuwa wakilia kwa kunyimwa mikataba mingi ambayo Serikali huingia na makampuni binafsi na hata wakiipata inaweza kuchelewa kujadiliwa na kufanya uamuzi juu ya suala hilo," alisema. Kutokana na hilo, Sungusia alipendekeza mabadiliko ya kifungu cha sheria kinacholazimisha usiri ili kandarasi ambazo Serikali inatia saini ziwekwe wazi na kuongeza uwajibikaji.
Kama umestaajabu uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM, kumteuwa Paul Makonda kuwa Katibu wake wa Itikadi
Kama umestaajabu uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM, kumteuwa Paul Makonda kuwa Katibu wake wa Itikadi na Uenezi, makada wa chama hicho na wanazuoni mbalimbali wanaeleza sababu za kwanini amekuwa yeye na si mwingine. Uamuzi wa uteuzi wa Makonda katika nafasi hiyo, kwa mujibu wa wanazuoni hao, umetokana na malengo ya chama hicho kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na uchaguzi mkuu wa 2025. Kwa upande mwingine, uteuzi wake ni tiba ya makundi yaliyozaliwa ndani ya chama hicho, ikidhaniwa Mikoa ya kanda ya ziwa wameacha katika nafasi za juu, ilhali ndiko kwenye mtaji mkubwa wa kura kama wanavyoeleza wachambuzi. Makonda ameteuliwa kushika wadhifa huo juzi, akimrithi Sophia Mjema aliyehudumu tangu Januari 14, mwaka huu alipoachiwa kijiti na Shaka Hamdu Shaka. Pamoja na wengi waliotabiri kuteuliwa kwake, lakini uteuzi wake uliibua mjadala mkali katika mitandao ya kijamii, wengi wakikosoa kwa rejea za utendaji wake alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Mwanaharakati, Fatma Karume ni miongoni mwa wakosoaji hao, aliyeandika katika ukurasa wake wa X, “Ina maana CCM haina mtu wa kusambaza itikadi zenu isipokuwa Makonda? Au hulka ya ubabe za Paulo (Makonda) inaendana na itikadi ya CCM? Mnaona Paul katulia, si mmempa nguvu subirini sasa muone.” Makundi Kuna hisia kuwa ujio wake kama ulivyokuwa katika uteuzi wa Dk Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu akishikilia wadhifa pia wa Waziri wa Nishati, una lenga kujenga ushawishi na kukubalika katika mikoa ya Kanda ya Ziwa. Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Kagera, Mara, Shinyanga, Simiyu, Geita na Tabora ndio inayotajwa kuwa na idadi kubwa ya wapiga kura inayoweza kuamua hatma ya chama gani kishike hatima ya uongozi katika uchaguzi mkuu. “Kanda ya ziwa ni muhimu sana kisiasa. Hata Chadema walifanya mikutano mingi kule na wanakubalika. Hii kwangu naona CCM inataka kujiimarisha na watu kama Makonda na Biteko wanatoka huko wanaweza kuisaidia,” alieleza mwana CCM. Kada huyo ambaye hakutaja kutajwa jina lake, alidai kulikuwa na dhana baada ya kifo cha Magufuli, kanda hiyo iliwekwa kando katika nafasi za maamuzi na kuona kama kulikuwa na kundi la Sukuma Gang, ambalo halionekani. Hoja hiyo, inaungwa mkono na mhadhiri wa sayansi ya siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe aliyesema uteuzi wake utatibu changamoto ya makundi na kuleta pamoja mtaji wa wapiga kura kutoka kanda ya ziwa. “Uteuzi wa Makonda unaweza kuwa tiba ya kuua makundi ndani ya CCM na kuleta pamoja mtaji mkubwa wa karibia asilimia 30 ya wapiga kura kutoka Kanda ya Ziwa,” alisema. Kulingana na mwanazuoni huyo, makundi ndani ya chama hicho yaliripotiwa zaidi hasa baada ya kifo cha Hayati Magufuli hasa lile la Sukuma Gang. “Kundi hili lilijinasibu na mtaji mkubwa wa wapiga kura toka mikoa ya kanda ya ziwa. Hata vyama vya upinzani utakumbuka vimewekeza sana kwenye eneo hili kwa kufanya mikutano mingi,” alisema Dk Kabobe. Hata hivyo, aliijenga hoja hiyo kwa ufafanuzi kuwa, makundi kwenye siasa si jambo ovu, lakini huwa baya pale linapotaka kukigawa chama husika na kuondoa umoja. Mrithi sahihi wa Nape, Polepole Mbali na mtazamo huo wa Dk Kabobe, baadhi ya makada wa CCM, wanaona hakukuwahi kupatikana mtu wa kuziba nafasi ya Humphrey Polepole aliyeshikilia wadhifa huo kati ya Desemba 2016 hadi Aprili 2021. Polepole alipokea kijiti kutoka kwa Nape Nnauye ambaye kwa sasa ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, huyu naye anatajwa kuwa miongoni mwa waliowahi kuutendea vema wadhifa huo. Baada ya Polepole, kiti hicho kilikaliwa na Shaka Hamdu Shaka hadi Januari 14, 2023 CCM ilipofanya mabadiliko na kumteua Sophia Mjema, ambaye amehudumu kwa siku 281 hadi Oktoba 22, 2023, kisha Makonda. “Ukweli ni kuwa tangu Polepole aondoke bado tulikuwa hatujapata mtu wa kuvaa viatu vyake kwa sababu Polepole alikuwa na uwezo wa kujibu hoja za wapinzani kweli kweli. Ngoja tuone Makonda naye,”alieleza Kada mmoja wa CCM. Historia yake Lakini sifa nyingine inayotajwa kumbeba Makonda ni historia yake ya kisiasa kuanzia Bunge la Katiba, ukuu wa wilaya na baadae RC Dar es Salaam, alionyesha uwezo mkubwa wa kiuongozi, ukiacha makando kando anayohusishwa nayo. Halikadhalika baadhi ya wachambuzi, wanachama wa CCM na wananchi wanamuona Makonda kama mmoja wa viongozi vijana na wenye ubunifu na mikakati, na sifa hiyo inaweza kukisaidia CCM katika mipango yake kuelekea 2025. Kujibu mapigo Kujibu mapigo katika hoja zinazoibuliwa na wapinzani hasa kipindi hiki ambacho mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa imeruhusiwa, ni jambo lingine lililompa turufu Makonda katika uteuzi huo kwa mujibu wa Dk Kabobe. “Namuona Makonda kama kijana na mwanasiasa anayeweza kumudu mikikimiki ya siasa za upinzani hasa kwa nafasi yake ya itikadi na uenezi,” alisema. Hata hivyo, gazeti hili limedokezwa kuwa CCM kimeamua Makonda kushika nafasi hiyo kama mtu anayeweza kujibizana majukwaani kwa hoja na makamu mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu anayeonekana kukisumbua CCM. Mjumbe mmoja wa NEC ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema Lissu amekuwa akimwaga sumu katika mikutano ya hadhara nchini na Makatibu waliomtangulia Makonda, walikuwa ‘wamepoa’ katika kujibizana na Lissu. Makonda anayo historia ya kukabiliana vilivyo na aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliohusisha vyama vya Chadema, NCCR- Mageuzi, CUF na NLD, Edward Lowassa, mashambulizi yaliyompa jina katika medani za siasa. Hulka ya Makonda kama kiongozi, ni jambo linalotajwa na Dk Kabobe kama sababu ya kuteuliwa kwa mwanasiasa huyo, akifafanua ni kiongozi mwenye uthubutu na asiye na woga. “Ukichilia mbali tuhuma anazokabiliwa nazo ambazo hazijawahi kuthibitishwa rasmi, Makonda ni kiongozi mwenye kuthubutu na hana woga hasa pale anapojua mamlaka iko upande wake. “Ana msimamo kwa anachokiamini hata kama sio sahihi kwa watu wengine,” alisema. Alisema Makonda ni kiongozi mwenye kutaka kuona matokeo sasa na sio kesho hata kama taratibu zilizopo haziruhusu atajitahidi kutumia mbinu mbadala ili aone matokeo. “Kwa hulka hii, CCM imepata mtu sahihi wa kukabiliana na changamoto za usimamizi wa miradi ya maendeleo iliyoko kwenye ilani ya 2020/25,” alisema. Lingine lililombeba, kwa mujibu wa Dk Kabobe ni aina yake ya uongozi wa kupenda kazi yake ionekane kwa watu hasa kwa kutumia vyombo vya habari. “Utakumbuka alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitumia sana vyombo vya habari kutatua changamoto za watu hadi wakati mwingine alionekana akipigiwa simu na mamlaka “live” kuonesha kuwa anachofanya mamlaka inakiunga mkono,” alisema. Alieleza kazi inayofanywa na CCM inahitaji kutangazwa kwa umma na kama Makonda akiendeleza tabia yake ya kutaka mambo yaonekane, basi uteuzi wake unaweza kuwa sahihi. Kinachomkabili Mwanazuoni huyo alisema tuhuma mbalimbali dhidi ya mwanasiasa huyo ndiyo mtihani mkubwa unaomkabili na kwamba anapaswa kuzisafisha. “Atapaswa kusafisha uwanja juu yake mwenyewe kuhusu tuhuma ambazo tumeziskia mara nyingi. Kumbuka kuna msemo usemao mke wa mfalme hapaswi kutuhumiwa,” alisema. Alisema mwanasiasa huyo atakabiliwa na dhana za baadhi ya watu kuwa, kuteuliwa kwake maana yake utawala uliopita umerejea. “Hii inaweza kuwa changamoto kwake hasa ndani ya chama chake,” alisema.
Uteuzi wa Paul Makonda kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM ndio habari ya mjini, kwani mijadala ni
Uteuzi wa Paul Makonda kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM ndio habari ya mjini, kwani mijadala ni mizito lakini wadau wa siasa wanataja sifa tano zilizombeba huku uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025 ukitajwa. Wadau hao wanaona kwa aina ya siasa za ushindani mkali wa Tanzania kwa sasa na baada ya kuondoka kwa Rais wa awamu tano, John Magufuli, anayeweza kuwa na mikakati sahihi ya kukivusha chama hicho, ni mtu wa aina ya Makonda. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na uchaguzi mkuu 2025 unatabiriwa kuwa na ushindani mkali, kama Katiba na sheria za uchaguzi zitabadilishwa ili kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi inayoliliwa na wadau wa demokrasia nchini. Makundi Mbali na sifa hiyo, lakini kuna hisia kuwa ujio wake kama ulivyokuwa katika uteuzi wa Dk Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu akishikilia wadhifa pia wa Waziri wa Nishati, una lenga kujenga ushawishi na kukubalika katika mikoa ya Kanda ya Ziwa. Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Kagera, Mara, Shinyanga, Simiyu, Geita na Tabora ndio inayotajwa kuwa na idadi kubwa ya wapiga kura inayoweza kuamua hatma ya chama gani kishike hatima ya uongozi katika uchaguzi mkuu. “Kanda ya ziwa ni muhimu sana kisiasa. Hata Chadema walifanya mikutano mingi kule na wanakubalika. Hii kwangu naona CCM inataka kujiimarisha na watu kama Makonda na Biteko wanatoka huko wanaweza kuisaidia,” alieleza mwana CCM. Kada huyo ambaye hakutaja kutajwa jina lake, alidai kulikuwa na dhana baada ya kifo cha Magufuli, kanda hiyo iliwekwa kando katika nafasi za maamuzi na kuona kama kulikuwa na kundi la Sukuma Gang, ambalo halionekani. Hoja hiyo, inaungwa mkono na mhadhiri wa sayansi ya siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe aliyesema uteuzi wake utatibu changamoto ya makundi na kuleta pamoja mtaji wa wapiga kura kutoka kanda ya ziwa. “Uteuzi wa Makonda unaweza kuwa tiba ya kuua makundi ndani ya CCM na kuleta pamoja mtaji mkubwa wa karibia asilimia 30 ya wapiga kura kutoka Kanda ya Ziwa,” alisema. Kulingana na mwanazuoni huyo, makundi ndani ya chama hicho yaliripotiwa zaidi hasa baada ya kifo cha Hayati Magufuli hasa lile la Sukuma Gang. “Kundi hili lilijinasibu na mtaji mkubwa wa wapiga kura toka mikoa ya kanda ya ziwa. Hata vyama vya upinzani utakumbuka vimewekeza sana kwenye eneo hili kwa kufanya mikutano mingi,” alisema Dk Kabobe. Hata hivyo, aliijenga hoja hiyo kwa ufafanuzi kuwa, makundi kwenye siasa si jambo ovu, lakini huwa baya pale linapotaka kukigawa chama husika na kuondoa umoja. Mrithi sahihi wa Nape, Polepole Mbali na mtazamo huo wa Dk Kabobe, baadhi ya makada wa CCM, wanaona hakukuwahi kupatikana mtu wa kuziba nafasi ya Humphrey Polepole aliyeshikilia wadhifa huo kati ya Desemba 2016 hadi Aprili 2021. Polepole alipokea kijiti kutoka kwa Nape Nnauye ambaye kwa sasa ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, huyu naye anatajwa kuwa miongoni mwa waliowahi kuutendea vema wadhifa huo. Baada ya Polepole, kiti hicho kilikaliwa na Shaka Hamdu Shaka hadi Januari 14, 2023 CCM ilipofanya mabadiliko na kumteua Sophia Mjema, ambaye amehudumu kwa siku 281 hadi Oktoba 22, 2023, kisha Makonda. “Ukweli ni kuwa tangu Polepole aondoke bado tulikuwa hatujapata mtu wa kuvaa viatu vyake kwa sababu Polepole alikuwa na uwezo wa kujibu hoja za wapinzani kweli kweli. Ngoja tuone Makonda naye,”alieleza Kada mmoja wa CCM. Historia yake Lakini sifa nyingine inayotajwa kumbeba Makonda ni historia yake ya kisiasa kuanzia Bunge la Katiba, ukuu wa wilaya na baadae RC Dar es Salaam, alionyesha uwezo mkubwa wa kiuongozi, ukiacha makando kando anayohusishwa nayo. Halikadhalika baadhi ya wachambuzi, wanachama wa CCM na wananchi wanamuona Makonda kama mmoja wa viongozi vijana na wenye ubunifu na mikakati, na sifa hiyo inaweza kukisaidia CCM katika mipango yake kuelekea 2025. Kujibu mapigo Kujibu mapigo katika hoja zinazoibuliwa na wapinzani hasa kipindi hiki ambacho mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa imeruhusiwa, ni jambo lingine lililompa turufu Makonda katika uteuzi huo kwa mujibu wa Dk Kabobe. “Namuona Makonda kama kijana na mwanasiasa anayeweza kumudu mikikimiki ya siasa za upinzani hasa kwa nafasi yake ya itikadi na uenezi,” alisema. Hata hivyo, gazeti hili limedokezwa kuwa CCM kimeamua Makonda kushika nafasi hiyo kama mtu anayeweza kujibizana majukwaani kwa hoja na makamu mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu anayeonekana kukisumbua CCM. Mjumbe mmoja wa NEC ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema Lissu amekuwa akimwaga sumu katika mikutano ya hadhara nchini na Makatibu waliomtangulia Makonda, walikuwa ‘wamepoa’ katika kujibizana na Lissu. Makonda anayo historia ya kukabiliana vilivyo na aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliohusisha vyama vya Chadema, NCCR- Mageuzi, CUF na NLD, Edward Lowassa, mashambulizi yaliyompa jina katika medani za siasa. Hulka ya Makonda kama kiongozi, ni jambo linalotajwa na Dk Kabobe kama sababu ya kuteuliwa kwa mwanasiasa huyo, akifafanua ni kiongozi mwenye uthubutu na asiye na woga. “Ukichilia mbali tuhuma anazokabiliwa nazo ambazo hazijawahi kuthibitishwa rasmi, Makonda ni kiongozi mwenye kuthubutu na hana woga hasa pale anapojua mamlaka iko upande wake. “Ana msimamo kwa anachokiamini hata kama sio sahihi kwa watu wengine,” alisema. Anapenda matokeo Alisema Makonda ni kiongozi mwenye kutaka kuona matokeo sasa na sio kesho hata kama taratibu zilizopo haziruhusu atajitahidi kutumia mbinu mbadala ili aone matokeo. “Kwa hulka hii, CCM imepata mtu sahihi wa kukabiliana na changamoto za usimamizi wa miradi ya maendeleo iliyoko kwenye ilani ya 2020/25,” alisema. Lingine lililombeba, kwa mujibu wa Dk Kabobe ni aina yake ya uongozi wa kupenda kazi yake ionekane kwa watu hasa kwa kutumia vyombo vya habari. “Utakumbuka alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitumia sana vyombo vya habari kutatua changamoto za watu hadi wakati mwingine alionekana akipigiwa simu na mamlaka “live” kuonesha kuwa anachofanya mamlaka inakiunga mkono,” alisema. Alieleza kazi inayofanywa na CCM inahitaji kutangazwa kwa umma na kama Makonda akiendeleza tabia yake ya kutaka mambo yaonekane, basi uteuzi wake unaweza kuwa sahihi. Kinakachomkabili Mwanazuoni huyo alisema tuhuma mbalimbali dhidi ya mwanasiasa huyo ndiyo mtihani mkubwa unaomkabili na kwamba anapaswa kuzisafisha. “Atapaswa kusafisha uwanja juu yake mwenyewe kuhusu tuhuma ambazo tumeziskia mara nyingi. Kumbuka kuna msemo usemao mke wa mfalme hapaswi kutuhumiwa,” alisema. Alisema mwanasiasa huyo atakabiliwa na dhana za baadhi ya watu kuwa, kuteuliwa kwake maana yake utawala uliopita umerejea. “Hii inaweza kuwa changamoto kwake hasa ndani ya chama chake,” alisema.
Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa DP World, Sultan Ahmed Bin Suleim amesema matarajio ya kampuni
Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa DP World, Sultan Ahmed Bin Suleim amesema matarajio ya kampuni hiyo ni kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa na ushindani wa kidunia. Suleim ameyasema hayo leo, Oktoba 22, 2023 alipohutubia wakati wa hafla ya kusainiwa kwa mikataba ya utekelezaji kati ya Serikali ya Tanzania na DP World katika bandari ya Dar es Salaam. Amesema kwa awamu tofauti, kampuni hiyo itahakikisha inaboresha huduma za usafiri na usafirishaji katika bandari ya Dar es Salaam. “Mkataba huu ni hatua nzuri kwa DP World katika kuendeleza uzoefu wake, lakini kuimarisha miundombinu ya bandari hii,” amesema. Amesema biashara ya Afrika kwa sasa ni chini ya asilimia 23, ni rahisi kuingiza kitu Afrika kutoka nje, kuliko kuingiza katika nchi jirani nyingine nje ya bara hilo. “Tunaamini mkataba huu utakomesha urasimu na vikwazo vyote vya biashara,” amesema. Ameeleza zipo namna mbalimbali ambazo Tanzania itanufaika hasa katika sekta za kilimo na ujenzi kupitia usafirishaji wa mazao yake. “DP World hatupo tu bandarini, tupo katika usafirishaji, bandari kavu, tunauzoefu, pia tunataka kutengeneza maeneo ya viwanda yatakazozalisha ajira lakini cha muhimu zaidi tutahakikisha Tanzania inasafirisha bidhaa zake zikiwa zimeshachakatwa na kuwa katika soko la dunia,” amesema.
Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda ndiye aliyeteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri
Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda ndiye aliyeteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi akimrithi Sophia Mjema. Makonda anaukwaa wadhifa huo akimrithi Sophia ambaye Rais Samia Suluhu Hassan amemteuwa kuwa mshauri wake wa masuala ya wanawake na makundi maalum. Ule msemo wa dunia duara, umeakisi uhalisia, Makonda (akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam) alikuwa bosi wa Daniel Chongolo (aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni) na sasa mambo yamekuwa kinyume. Ndani ya chama hicho, Chongolo ambaye ni Katibu Mkuu wa CCM, kwa sasa anakuwa bosi wa Makonda. Taarifa ya uteuzi wa Makonda, imetokewa leo Oktoba 22, 2023 na CCM muda mchache baada ya kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho. Kulingana na taarifa hiyo, pamoja na Makonda, mwingine aliyeteuliwa na NEC ni Rabia Abdallah Hamid kuwa Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. Rabia anamrithi, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Huyu ndiye Makonda Jina la Makonda lilitambulika mwaka 2014, alipokuwa mmoja wa wajumbe wa Kamati ya marekebisho ya Katiba. Wadhifa wake serikalini ulianzia katika Wilaya ya Kinondoni alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo. Baadaye, Hayati John Magufuli alimteuwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, eneo ambalo ndilo alilopatia umaarufu zaidi. Januari mwaka 2020, Marekani ilitangaza marufuku ya mwanasiasa huyo na familia yake kutoingia nchini humo, ikimtuhumu kuvunja haki za binadamu.
Rais Samia Suluhu Hassan amemteuwa Sophia Mjema kuwa Mshauri wake kwenye masuala ya Wanawake na Maku
Rais Samia Suluhu Hassan amemteuwa Sophia Mjema kuwa Mshauri wake kwenye masuala ya Wanawake na Makundi Maalum. Sophia anaukwaa wadhifa huo, akitoka kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi alioutumikia kwa miezi tisa. Uteuzi wa Mjema umetangazwa leo, Oktoba 22, 2023 kupitia taarifa kwa vyombo vya habari iliyotiwa saini na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus. Hata hivyo, Mjema anateuliwa kushika wadhifa huo mpya katikati ya wimbi la taarifa kuwa huenda CCM ikafanya mabadiliko katika wajumbe wa sekretarieti. Gazeti la Mwananchi hivi karibuni liliripoti juu ya kufanyika kwa kikao cha NEC ya dharura leo, ambayo pamoja na mambo mengine, inatarajiwa kuja na mabadiliko katika wajumbe wa sekretarieti ya CCM. Mbali na mabadiliko hayo, ajenda nyingine kulingana na vyanzo ambavyo gazeti la Mwananchi limevinukuu, kikao hicho kitajadili kuhusu mikataba wa uendelezaji na uboreshaji wa bandari ya Dar es Salaam, kati ya Serikali ya Tanzania na DP World ya Dubai. Kwa muktadha huo, uteuzi mpya wa Mjema ni kama umeanza kujibu kile kilichoelezwa na vyanzo mbalimbali ambavyo Mwananchi imekuwa ikivinukuu. Huyu ndiye Mjema Kujulikana kwake katika siasa, kulianza mwaka 2005 alipowania ubunge wa viti maalum katika Mkoa wa Kilimanjaro, hata hivyo hakufanikiwa alishika nafasi ya tano. Milango ya kuyaishi maisha ya siasa, ilimfungukia mwaka 2006, alipoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete wa wakati huo, kuwa Mkuu wa Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga. Utumishi wake katika wadhifa huo, ulikoma mwaka 2012, alipohamishiwa wilayani Temeke na baadaye Ilala. Uamuzi wake wa kuwania ubunge katika Jimbo la Ilala, ulimtenganisha na wadhifa huo, lakini baadaye Oktoba 8, 2021 aliteuliwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Hata hivyo, miaka miwili baadaye aliteuliwa kuwa sehemu ya sekretarieti ya CCM, Januari 14, mwaka huu.
Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango ametoa siku 14 kwa Wizara ya Uchukuzi na Wizara ya Fedha, kuchunguz
Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango ametoa siku 14 kwa Wizara ya Uchukuzi na Wizara ya Fedha, kuchunguza na kutoa suluhu ya gharama kubwa za usafirishaji mizigo kupitia ndege ya mizigo ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL). Malalamiko ya gharama hizo, yaliibuliwa na Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi aliyesema baadhi ya wasafirishaji wanashindwa kuitumia ndege hiyo kutokana na ukubwa wa gharama. "Baadhi ya wasafirishaji wanashindwa kutumia ndege yetu katika baadhi ya viwanja, kikiwemo cha Kilimanjaro kutokana na gharama za usafirishaji kuwa kubwa. "Zinasababishwa na mlolongo wa tozo na kodi, pia miundombinu duni ya viwanja vetu ukilinganisha na washindani wetu," alisema. Dk Mpango, alitoa maagizo hayo jijini Dar es Salaam jana, alipohutubia hafla ya mapokezi ya ndege aina ya Boeing 737-9 Max kutoka Marekani hadi nchini. Katika hotuba yake hiyo ya takriban dakika 40, alizitaka wizara hizo zichunguze ili kubaini kiini cha tatizo kisha ziwasilishe mapendekezo serikalini. "Hebu mfanye uchambuzi wa uhakika na mlete maoendekezo serikalini, mnafahamu vema kwamba tumewekeza fedha nyingi kununua ndege hizo na lengo letu ni kuongeza shehena ya mizigo," alisema. Katika maelekezo yake hayo, Dk Mpango alitaka yatekelezwe kwa siku 14 kuanzia jana. Mengine kuhusu ndege hiyo ya mizigo, Mhandisi Matindi aliaema kati ya Julai na Agosti mwaka huu imebeba jumla ya tani 337 na matarajio ni kubeba tani 4,800 kufikia Juni mwaka 2024. Kuchelewa, kuahirishwa safari Katika hotuba yake, Dk Mpango alitaja kuwepo malalamiko ya kuahirishwa na kucheleweshwa safari za ndege za ATCL, akitaka ikome baada ya kuwasili kwa ndege hiyo. "Bado kuna malalamiko ya wateja kuhusu kuahirishwa kwa safari au kusogeza muda wa safari mbele, kelele zaidi zipo Uwanja wa ndege wa Mwanza. "Baada ya kupokea ndege hii mpya, matarajio ya wengi ni kwamba tatizo hilo litakwisha," alisema. Lakini, aliitaka Wizara ya Uchukuzi kusimamia utoaji huduma wa ATCL ili kuimarisha ushindani wa kikanda na kuongeza pato la taifa. "Fanyeni kazi kibiashara kwa kuzingatia sheria za usafiri wa anga," alisema. Kuhusu bidhaa za viburudishi vya ndani ya ndege, Dk Mpango alitaka manunuzi yazingatie zinazotoka nchini. Kadhalika, alitaka shirika hilo lisimamiwe ili kulinda mtaji uliowekezwa na Watanzania. "Serikali haitavumilia tena uzembe kama iliyotokea katika miaka ya nyuma," alisema Kuhusu ndege za mafunzo za NIT, alisema mwaka 2021 Serikali ilikiwezesha chuo hicho kuingia mkataba wa ununuzi wa ndege mbili kutoka kampuni ya Textron Aviation Inc ya Marekani. Alisema tayari Serikali imetoa fedha kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uhandisi wa matengenezo ya ndege, uhudumu wa ndege kwa ithibati za Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) katika chuo hicho. Ili kuongeza ufanisi wa NIT, alisema Juni mwaka huu Serikali imekiwezesha chuo hicho kununua ndege nyingine yenye injini mbili inayotarajiwa kuwasili katika robo ya tatu ya mwaka ujao. Aliitaka bodi ya chuo hicho ihakikishe ndege hizo zinatunzwa na kuzingatia masuala ya usalama ili zitoe mafunzo kwa muda mrefu. Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisema ndege ya ATCL iliyowasili jana ina uwezo wa kubeba mizigo ya tani sita. Ujio wake, alisema utaongeza mtandao wa safari za ndege za ATCL na kuwa chachu ya kutanuka kwa biashara. "Hii itasaidia ukuaji wa sekta ya biashara, uchumi, afya kwani baadhi ya watu wanakuja kupata huduma za afya nchini," alisema. Kuhusu ndege za mafunzo za NIT, alisema zitatatua changamoto ya uhaba wa marubani nchini. Alieleza Wizara hiyo itaendelea kujenga mazingira wezeshi kwa taasisi zilizopo chini yake ikiwemo ATCL na NIT. "Wizara imeendelea kuhakikisha tunakuwa na viwanja bora na miundombinu itakayokuza biashara," alisema. Alisema kwa Uwanja wa Dodoma huduma za usafiri wa anga zitaanza kutolewa kwa saa 24 kuanzia jana. Lakini, alisema ufungaji wa taa za kuongozea ndege umeendelea kufanywa katika viwanja vya Ndege mbalimbali ili vikidhi kufanya shughuli kwa saa 24. Ukodishaji ndege Kulingana na Profesa Mbarawa, kufikia Novemba mwaka huu, Serikali inatarajiwa kukamilisha mchakato wa kuhamisha umiliki wa ndege kutoka Wakala wa Ndege za Serikali kwenda ATCL. "Hii itaongeza mtaji wa ATCL na kuipunguzia gharama za uendeshaji, hoja ambayo ilitolewa pia na Mhandisi Matindi alipotoa hotuba yake. Awali, katika hotuba yake, Mhandisi Matindi alisema uamuzi wa kuhamisha umiliki wa ndege kutoka Wakala wa Ndege za Serikali hadi ATCL una tija kubwa katika kuimarisha mizania za hesabu na upatikanaji wa faida. Mhandisi Matindi alisema ujio wa ndege hiyo utaifanya ATCL kuwa na jumla ya ndege 14 na kwamba nyingine nbili zinatarajiwa kuingia nchini. Kati ya mbili hizo, alisema moja inatarajiwa kuwasili Novemba au mwishoni mwa mwaka huu na nyingine mwakani. Alieleza kumekuwa na ongezeko la abiria kutoka 106,138 mwaka 2016/17 hadi milioni 1.78 mwaka 2022/23 Kuhusu ndege hiyo mpya, alisema ina uwezo wa kubeba abiria 181 kati yao 16 ni katika daraja la biashara. Alisema ina uwezo wa kuruka masaa nane bila kutua na kwamba tayari ATCL imeshajiandaa. Kwa sasa, aliaema wanatoa huduma katika vituo 15 ndani ya nchi na 13 nje ya nchi. Alisema wanatarajia kuongeza miruko ya Mumbai, India na Guangzhou China, huku maandalizi ya kwenda Maskati na Ujerumani yakiratibiwa. Alipendekeza kuongezwa kwa ndege nyingine ya mizigo ili kuongeza ufanisi wa ile iliyopo. "Ili Ndege ya mizigo itumike kwa tija, Serikali inapaswa kuacha mchakato wa kununua ndege ya mizigo kwa ajili ya usafirishaji wa mizigo katika nchi jirani na kuijaza hii ya ndani," alisema. Kuhusu idadi ya marubani, alisema kwa sasa wameongezeka kutoka 11 hadi 105 na wahandisi 150 hadi 270 tangu kuanza utekelezaji wa mpangokazi wa ATCL mwaka 2016. Changamoto Alisema shirika hilo, alisema linakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa vipuli na matengenezo ya injini yanayofanywa na waundaji wake. Alisema tayari mkakati umeundwa kuhakikisha wanakuwa na kampuni watakazoshirikiana nazo kuazimana vipuri. Mwishi Hivi unajua kuwa Zanzibar ina jumla ya hoteli 710 zenye madaraja tofauti, kati ya hizo 38 ni hoteli zenye hadhi ya nyota tano. Idadi hiyo ya hoteli Zanzibar ndiyo inayoifanya kuwa miongoni mwa nchi zenye mvuto wa utalii wa mikutano, makongamano na maonyesho (MICE). Kulingana na Baraza la Utalii Duniani, thamani ya utalii wa mikutano Afrika ni Dola za Marekani 13 bilioni (zaidi ya Sh32.5 trilioni), ikiwa ni asilimia mbili ya thamani ya utalii huo duniani. Takwimu hizo za baraza la utalii ni kielelezo kuwa, fursa hiyo ya utalii haijachangamkiwa zaidi katika nchi za Afrika, hivyo inabaki kuwa turufu muhimu kwa uchumi, iwapo itatokea nchi itakayoichangamkia. Hicho ndicho kinachofanywa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, hasa katika kipindi cha miaka mitatu tangu kuingia madarakani kwa Rais Dk Hussein Ali Mwinyi. Tangu kuingia kwake madarakani akiiwakilisha Serikali ya awamu ya nane visiwani humo, ameweka mikakati madhubuti kuhakikisha utalii huo unakuwa miongoni mwa nyenzo ya uchumi wa Zanzibar. Katika mazungumzo yake na gazeti hili, Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Simai Mohammed Said anasema msukumo wa utalii huo katika visiwa hivyo, unatokana na kuwa sehemu ya maelekezo ya Ilani ya CCM ya mwaka 2020. Kadhalika, anasema utalii wa mikutano upo katika Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2050 na Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar (ZADEF) wa 2020/25. Si hivyo tu, anasema utalii wa mikutano ni miongoni mwa maagizo ya Rais wa Zanzibar, Dk Mwinyi kwani aliahidi kwa wananchi. Mipango hiyo, kwa mujibu wa Said, imeimarisha utalii huo ambapo sasa Zanzibar imekuwa ikiandaa mikutano mbalimbali ya wakuu wa nchi, mawaziri, mikutano ya kikanda na taasisi za kimataifa. “Hali hii imetokana na kuwepo kwa hoteli zenye hadhi na kumbi kubwa kwa mikutano zinazokubalika kimataifa. Ubora wa mazingira pia unaongeza mvuto katika kumbi hizo kwani nyingi zipo pembezoni mwa fukwe,” anasema. Ilivyojipanga Ili kufikia adhma ya Zanzibar kuwa kitovu cha utalii wa mikutano, anasema hekta 60 zimetolewa na Serikali kwa mwekezaji katika eneo la Nyamanzi kwa ajili ya kujenga ukumbi mkubwa wa mikutano, utakaoizidi mingine ya Afrika Mashariki. “Kufikia mwaka 2025 Zanzibar itakuwa ikiongoza kwa kuwa na ukumbi mkubwa wa mikutano Afrika Mashariki,” anasema. Anafafanua ukumbi huo utakuwa na uwezo wa kuchukua watu 1,500 hadi 2,000 kwa wakati mmoja, kadhalika utahusisha kumbi ndogo za mikutano. Mtindo wa ukumbo huo, kwa mujibu wa Said, utajengwa kuendana na kumbi za Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola na aina nyingine ambazo zimebainika kuwa na soko duniani. “Kwa ufupi Zanzibar itakuwa kituo kikuu cha mikutano ya kimataifa kwa bara la Afrika,” anasema. Anaeleza kwa sasa, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda, Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale zinaendelea na hatua za ufanikishwaji wa utekelezaji wa mradi huo. “Hivi sasa kuna timu ipo katika safari maalum ya kikazi nchini Korea Kusini kufuatiolia hatua za ujenzi wa ukumbi huo,” anasema. Si ukumbi pekee, Said anasema ujenzi wa hoteli mpya ya Emarald iliyopo Matemwe unakaribia kukamilika na ndani yake kutakuwa na ukumbi utakaokuwa na uwezo wa kuchukua watu 1,000, unaotarajiwa kuimarisha utalii wa mikutano visiwani humo. Anasema hamasa inatolewa kwa wawekezaji mbalimbali visiwani humo, wanapojenga hoteli wahakikishe zinakuwa na kumbi kubwa za mikutano kwa kuwa soko la utalii wa mikutano ni kubwa visiwani humo. Mbali na kumbi, Said anasema yapo maeneo ya nje ambayo mikutano mbalimbali hufanyika na kwamba Serikali imeshayawekea mkakati wa kuyaboresha. Utalii wa mikutano kabla na baada ya Mwinyi Said anasema utalii wa mikutano ulikuwepo tangu kabla ya Rais Mwingi aingie madarakani, ingawa haukuwa na msikumo kama uliopo sasa. Anasema msukumo huo umesababisha kuongezeka kwa idadi ya mikutano katika visiwa. “Tangu Rais Dk Mwinyi aingie madarakani hazipitia siku tatu hapa Zanzibar kusifanyike mikutano wa kimataifa, ni jambo linaloshuhudiwa na kila mtu,” anasema. Kabla ya hapo, anasema mikutano kama hiyo ilifanyika kwa nadra na kilichowavutia waandaaji ilikuwa ni mandhari ya visiwa hivyo, lakini sasa wizara yake inasimamia kutangaza fursa na vivutio vya utalii na hivyo kuwavutia wengi. “Kwa sasa wizara imelivalia njuga suala la kutangaza utalii na inatumia njia zote katika maonyesho ya kitaifa na kimataifa na njia za mitandaoni,” anasema. Sekta ya utalii, anasema inachangia asilimia 29.2 katika pato la taifa la Zanzibar ndiyo maana Rais Mwinyi ameupa nafasi kubwa katika uchumi. “Utalii wa Mikutano unakuza uwekezaji na unazalisha ajira nyingi, hivyo Dk Mwinyi amekuwa akiielekeza Wizara ya Utalii kutumia nguvu nyingi katika kuvuna fursa hii, ikizingatiwa kuwa utalii wa fukwe, jua na mchanga mzuri tayari umeshatangazwa na ni bidhaa yenye ushindani inayopatikana katika visiwa vingine pia, lakini mazingira ya mikutano yaliyopo Zanzibar ni tunu kwengineko ulimwenguni,” anasema. Hali ya amani, usalama na utulivu katika visiwa hivyo iliyoimarika katika utawala wa Dk Mwinyi, anasema ni turufu nyingine katika soko la utalii wa mikutano. Kulingana na Said, ni mikutano mingi imefanyika visiwani humo tangu kuingia madarakani kwa Dk Mwinyi, ingawa ni vigumu kuhesabika. “Mikutano hiyo imeongezeka kwa sasa kiasi cha kuonekana kama ndio kivutio kikuu cha utalii kwa Zanzibar,” anasema. Anasema katika visiwa hivyo, aina zote za mikutano hufanyika ikiwemo ile yenye washiriki wenye ukubwa au vyeo au unyeti na mingine inayofanywa na taasisi kubwa. “Kuna mikutano inayoshirikisha watu wachache ila ni mikubwa kutokana na hadhi ya washiriki wake ambao hufuata unyeti wa kumbi za Zanzibar kwa kufanyika mikutano ya watu wazito kama wao. “Kumbi za aina hiyo zipo katika hoteli za Zanzibar nyingi mno.” anasema. Anasema mikutano mingine inayofanyika ni ile ya taasisi kubwa za Kimataifa kama Umoja wa Mataifa (UN) na taasisi zilizo chini yake. “Zanzibar imekuwa New York ndogo kwa kufanyika vikao vingi vya taasisi hizo kwa Afrika Mashariki,” anasema. Kwa mujibu wa Said, mikutano ya benki, mashirika mengine ya kitaifa, yote imekubali katika kipindi cha miaka mitatu ya Dk Mwinyi, imekubali Zanzibar kuwa ndio kituo chao cha mikutano. “Hili limefanyika kwa Mheshimiwa Rais mwenyewe kuwaalika rasmi kutumia kumbi za mikutano za Zanzibar,” anasema. Anaeleza tayari kuna mikutano mikubwa iliyothibitishwa kufanyika katika visiwa hivyo mwaka 2024, ikiwemo Mkutano wa Mawaziri wa Sheria wa Nchi za Jumuiya ya Madola utakaofanyika Machi 5-8 mwakani. “Mikutano mingine mikubwa ya kitalii pia nayo itafanyika mwaka 2024 na mingine iliyofanyika mwaka 2023 itafanyika tena mwaka 2024,” anasema.
Serikali imethibitisha kuilipa kampuni ya Winshear Gold Sh75 bilioni kama stahiki yake, baada ya maz
Serikali imethibitisha kuilipa kampuni ya Winshear Gold Sh75 bilioni kama stahiki yake, baada ya mazungumzo nje ya mahakama. Taarifa za malipo hayo yaliyofanywa na Serikali ya Tanzania kwa Winshear zilitolewa juzi na kampuni hiyo, ikifafanua ni sehemu ya fidia baada ya kumaliza migogoro baina ya pande hizo mbili. Mzizi wa mgogoro huo ni Serikali kuifutia kampuni hiyo leseni ya uendeshaji wa mradi wa dhahahu wa SMP na katika kujibu mapigo Winshear ilishitaki. Uamuzi huo wa Serikali kufuta leseni ulitokana na mabadiliko ya sheria ya madini ya mwaka 2010, ambapo kanuni zake zilifuta leseni hizo. Katika taarifa yake kwa umma juzi, Winshear iliweka wazi kuwa mgogoro huo umetamatika kwa Serikali kuilipa kiasi hicho cha fedha. Akizungumza kupitia taarifa huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Winshear, Richard Williams alisema hatua hiyo ni nzuri kwa pande zote. "Ni wakati mzuri wa pande zote kuendelea na mambo yake na tunaitakia Tanzania mafanikio katika kuvutia uwekezaji mpya," alisema. Katika taarifa huo, Williams alipongeza mawakili waliosimamia kesi hiyo. Alipotafutwa juzi kuzungumzia hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Eliezer Felesh alikiri kutokea ingawa hakufafanua kwa kina. Majibu ya Dk Felesh yalitokana na kuulizwa kuhusu taarifa ya Winshear iliyokuwa ikisambaa mtandaoni ambapo alijibu, "ndiyo ni kweli." Hata hivyo, Gazeti hili lilizungumza na Wakili Mkuu wa Serikali, Dk Boniface Luhende kutaka kujua undani wa kesi hiyo, aliyeelekeza atafute Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Alipotafutwa tena kufafanua hilo, Dk Feleshi simu yake iliita bila majibu. Hii si kesi ya kwanza Serikali inashindwa na kutakiwa kulipa mabilioni ya fidia. Julai mwaka huu, Serikali ilitakiwa kulipa fidia ya Sh260 bilioni kwa kampuni ya Indiana Resources iliyoshinda kesi katika mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji (ICSID), baada ya kujiridhisha ukiukwaji wa mkataba wa uwekezaji katika mradi wa Nikel wa Ntaka Hill mwaka 2018. Uamuzi kama huo pia, ulitolewa na ICSID mwaka 2019 ukiiamuru Serikali kuilipa kampuni ya IPTL fidia ya Sh426 bilioni kwa ukiukwaji wa masharti ya mkataba.
Singida ni miongoni mwa Mikoa yenye umri mkubwa nchini ikiwa ya mwanzo kuanzishwa baada ya muungano
Singida ni miongoni mwa Mikoa yenye umri mkubwa nchini ikiwa ya mwanzo kuanzishwa baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ulianzishwa Oktoba 15, 1963 mwaka mmoja baada ya kupatikana kwa jina la Tanzania lililotokana na muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ukongwe wake umebebwa na historia maridhawa ambayo kimsingi inaakisi mengi yanayoihusu Tanzania. Mkoa huo ulizaliwa baada ya kugawanywa kwa Jimbo la Kati ambalo pia limeuzaa Mkoa wa Dodoma, ulikuwa kigingi cha Wajerumani enzi hizo. Kulingana na duru mbalimbali Singida ndiko kulikokuwa na upinzani mkubwa katika vita dhidi ya wakoloni kutoka Ujerumani. Lakini yote hayo, yanabaki kuwa historia nzuri tu, huku Singida yenyewe ikiwa na changamoto lukuki. Pamoja na ukongwe wake, Singida unabaki kuwa miongoni mwa Mikoa mitano masikini nchini ukishika nafasi ya tano kutoka ile ya chini. Maswali ya wengi ni kwanini ukongwe haukuisaidia Singida kukomaa kwa maendeleo na uchumi. Au ndiyo tuseme mvi sio kipimo cha ukongwe wake? Singida yenye fursa lukuki za ardhi ya kilimo, ufugaji na madini, bado inabaki kuwa na hali mbaya kiuchumi. Mchango wa Singida katika pato la taifa ni asilimia mbili ikiwa ni miongoni mwa michango midogo inayochangiwa na Mikoa katika GDP. Mkoa unaoongoza ni Dar es Salaam ukichangia asilimia 17 katika pato la taifa. Kinachonishangaza ni sababu za vikwazo vya maendeleo katika Mkoa huo licha ya fursa ulizonazo. Hivi ni kweli imechukua miaka 60, Singida kuchangia asilimia mbili katika pato la taifa? Kuna haja ya kutafuta mzizi wa tatizo ili kama ni mabadiliko yafanyike au hatua zichukuliwe kubadilisha hali iliyopo. Naamini tatizo si viongozi waliopo katika Mkoa huo, kwa kuwa wamepita watu mbalimbali kuiongoza Singida ina maana Kati yao hakukuwa hata na mmoja aliyefanya vizuri. Bila shaka ipo shida nyingine inayosababisha hali iliyopo katika Mkoa huo na muhimu zaidi ni kuangalia tabia za watu na mtindo wao wa maisha. Tusiruhusu Mikoa yenye historia ikawa na midororo inayoweza kuathiri hata historia iliyonayo ni muhimu. Kama kuna kamati zinaundwa kwa ajili ya kushughulikia mambo mbalimbali ni muhimu kuundwe kamati pia kwa ajili ya kuchunguza changamoto za maendeleo katika Mkoa wa Singida
Serikali imethibitisha kuilipa kampuni ya Winshear Gold Sh75 bilioni kama stahiki yake, baada ya maz
Serikali imethibitisha kuilipa kampuni ya Winshear Gold Sh75 bilioni kama stahiki yake, baada ya mazungumzo nje ya mahakama. Taarifa za malipo hayo yaliyofanywa na Serikali ya Tanzania kwa Winshear zilitolewa juzi na kampuni hiyo, ikifafanua ni sehemu ya fidia baada ya kumaliza migogoro baina ya pande hizo mbili. Mzizi wa mgogoro huo ni Serikali kuifutia kampuni hiyo leseni ya uendeshaji wa mradi wa dhahahu wa SMP na katika kujibu mapigo Winshear ilishitaki. Uamuzi huo wa Serikali kufuta leseni ulitokana na mabadiliko ya sheria ya madini ya mwaka 2010, ambapo kanuni zake zilifuta leseni hizo. Katika taarifa yake kwa umma juzi, Winshear iliweka wazi kuwa mgogoro huo umetamatika kwa Serikali kuilipa kiasi hicho cha fedha. Akizungumza kupitia taarifa huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Winshear, Richard Williams alisema hatua hiyo ni nzuri kwa pande zote. "Ni wakati mzuri wa pande zote kuendelea na mambo yake na tunaitakia Tanzania mafanikio katika kuvutia uwekezaji mpya," alisema. Katika taarifa huo, Williams alipongeza mawakili waliosimamia kesi hiyo. Alipotafutwa juzi kuzungumzia hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Eliezer Felesh alikiri kutokea ingawa hakufafanua kwa kina. Majibu ya Dk Felesh yalitokana na kuulizwa kuhusu taarifa ya Winshear iliyokuwa ikisambaa mtandaoni ambapo alijibu, "ndiyo ni kweli." Hata hivyo, Gazeti hili lilizungumza na Wakili Mkuu wa Serikali, Dk Boniface Luhende kutaka kujua undani wa kesi hiyo, aliyeelekeza atafute Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Alipotafutwa tena kufafanua hilo, Dk Feleshi simu yake iliita bila majibu. Hii si kesi ya kwanza Serikali inashindwa na kutakiwa kulipa mabilioni ya fidia. Julai mwaka huu, Serikali ilitakiwa kulipa fidia ya Sh260 bilioni kwa kampuni ya Indiana Resources iliyoshinda kesi katika mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji (ICSID), baada ya kujiridhisha ukiukwaji wa mkataba wa uwekezaji katika mradi wa Nikel wa Ntaka Hill mwaka 2018. Uamuzi kama huo pia, ulitolewa na ICSID mwaka 2019 ukiiamuru Serikali kuilipa kampuni ya IPTL fidia ya Sh426 bilioni kwa ukiukwaji wa masharti ya mkataba.
Rais Samia Suluhu Hassan ametaka upendo, mshikamano na umoja kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Rais Samia Suluhu Hassan ametaka upendo, mshikamano na umoja kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024, akisema hatua hiyo itatoa taswira ya uchaguzi mkuu wa 2025. Katika kauli yake hiyo, Rais Samia amewasihi wanachama wa CCM kuepuka kukibomoa chama hicho na kuunda makundi kwa sababu ya kukosa nafasi watakazogombea. Rais Samia alitoa kauli hiyo mkoani Singida jana, alipozungumza na wananchi wa Wilaya ya Mkalama muda mchache baada ya kuzindua daraja la Msingi wilayani humo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake katika Mkoa huo. Katika hotuba yake hiyo, alisema alionya mambo mawili likiwemo lile la kuepuka makundi baada ya uchaguzi huo. “Uchaguzi una mkono wa Mungu inawezekana unataka sana kuchukua hiyo nafasi, lakini Mungu anakuwa hajakupangia, kwa hiyo unapokosa sasa tusianze kutengeneza makundi, tukaanza kukobomoa chama chetu, tukaanza kufanya maendeleo yasipatikane, tukaanza kufanya chuki, hapana huko tusifike,” alisema. Alisisitiza kudumishwa kwa umoja, mshikamano na upendo katika uchaguzi huo, ili utoe sura ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Mbali na makundi, Rais Samia aliwataka wananchi kuhakikisha wanawachagua viongozi watakaowatumikia. “Tunaelekea kwenye uchaguzi mwakani, tutakuwa na uchaguzi wa Serikali za Mitaa, niwaombe sana kwenye jambo hili kuweka watu watakaowatumikia, msiende kuweka watu watakaopitisha watu wengine. “Kama mnachagua watu katika ngazi za uchaguzi ule wekeni watu mnaojua hawa watakuja watutumikie wana Mkalama,” alisema. Kuhusu Singida Akiwa mkoani Singida katika maadhimisho ya miaka 60 ya Singida, Rais Samia alisema pamoja na umri huo, lakini mkoa huo ni miongoni mwa Mikoa msikini nchini. “Mkoa huu unachangia chini ya asilimia mbili kwenye pato la taifa na kuendelea kuwa miongoni mwa Mikoa mitano masikini zaidi nchini, lakini fursa alizotuumbia Mungu ni nyingi mno,” alisema. Alisema rasilimali na jiografia ya Singida inawezekana kuwa na mafanikio zaidi ya iliyonayo sasa. Alieleza changamoto zilizopo katika Mkoa huo ni mabadiliko ya tabianchi yanayoufanya kuwa miongoni mwa Mikoa inayopokea kiasi kidogo cha mvua, ukilinganisha na mingine. “Nakumbuka Singida ulikuwa miongoni mwa Mikoa inayopewa msaada wa chakula kwa sasa juhudi za viongozi zimeondoa hilo,” alisema. Kwa mujibu wa Rais Samia, kuna haja ya kuangalia mabadiliko ya tabia za watu ili watumie fursa zilizopo kwa maendeleo ya Mkoa huo. “Mfano vituo vya afya, Serikali imejenga lakini kwa sababu zisizoeleweka zaidi ya vituo 15 vimechelewa kufunguliwa, hii huwezi kusema chochote isipokuwa ni tabia za watu,” alisema. Rais Samia alitumia jukwaa hilo kuwasihi wananchi kujipanga kuepuka athari za mvua za El Nino zilizotabiriwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Historia ya Singida Akitoa historia ya kuanzishwa kwa Mkoa huo, Mbunge wa Kilosa, Profesa Palamagamba Kabudi alisema ulianzishwa Oktoba 15, mwaka 1963. Chimbuko la kuanzishwa kwake, alisema ni kugawanywa kwa Jimbo la Kati, lililozaa Singida na Mkoa wa Dodoma. Kulingana na Profesa Kabudi, asili ya jina la Singida ni jamii ya wataturu waliofika katika eneo hilo miaka ya 1500, wakiliita ‘Singieda Moheda’ lenye maana ya mbuga ya pundamilia. Jina hilo, lilitokana na kile alichofafanua, enzi hizo Singida ilikuwa mbuga yenye pundamilia wengi zaidi. Alisema jina Singieda Moheda liliwashinda wanyaturu waliofika eneo hilo wakitokea Ethiopia mwaka 1700 na hivyo wakaita Singida na ndilo lililopo hadi sasa. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa alisema serikali bado inafanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya elimu kwa kutenga bajeti ambapo ndani ya kipindi cha miaka miwili na nusu shule za msingi 302 zimejengwa. “Shule za kawaida zaidi ya 3000 zimejengwa , shule za awali 364, shule za sekondari shule 543 nchi nzima na katika mkoa huu wa Singida shule nyingi zimejengwa,”alisema Alisema Serikali inakusudia kuiboresha manispaa ya mkoa wa Singida kuiweka katika kiwango kinachoendana na hadhi ya miji kwa kujenga masoko, madaraja, barabara za lami na ujenzi wa taa za barabarani. Kuhusu daraja la Msingi Awali, akitoa taarifa ya mradi wa daraja la Msingi, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mohammed Besta alisema Sh11.1 bilioni zimetumika kufanikisha shughuli hiyo. Alieleza fedha hizo zimetolewa na Serikali na hata rasilimali watu iliyotumika katika ujenzi huo inatoka nchini. Kulingana na Besta, daraja hilo lipo katika barabara ya Mkoa na linaunganisha kati ya Singida, Simiyu, Mara na Arusha. “Ujenzi wa mradi huu, ulisimamiwa na taasisi ya usimamizi wa ujenzi wa madaraja na barabara kutoka Tanroads inaitwa TECU,” alisema Besta.
Huenda suala la kupanda kwa bei ya mbegu za mahindi nchini likafika mwisho, baada ya Serikali kuweka
Huenda suala la kupanda kwa bei ya mbegu za mahindi nchini likafika mwisho, baada ya Serikali kuweka mkakati wa kutangaza bei elekezi ya bidhaa hiyo kwa wakulima. Uamuzi wa kutangazwa kwa bei hizo, kwa mujibu wa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe unatarajiwa kufanywa Oktoba 20, mwaka huu. Haja ya kutangazwa kwa bei hizo, Bashe amesema ni uwepo wa kampuni binafsi zinazopandisha bei ya mbegu za mahindi kinyume na makubaliano ya leseni na kwamba itakayopandisha baada ya siku hiyo itafutiwa leseni. Kauli kuhusu kupandishwa kwa bei hiyo, iliibuliwa na wananchi wa Kateshi mkoani Manyara mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan aliposimama kuwasalimia wananchi wa eneo hilo akielekea Mkoa wa Singida kwa ziara ya kikazi. Katika safari hiyo jana, Rais Samia alimpa nafasi Bashe ya kulizungumzia suala hilo kujibu malalamiko ya wananchi akisema, “mheshimiwa waziri (Bashe) kabla hujateremka kuna kilio pale kuhusu mbegu.” Akifafanua hilo, Bashe alisema tayari ameshatoa maelekezo ya kutangazwa kwa bei elekezi ya mbegu na Oktoba 20, mwaka huu wakulima watazisoma magazetini. Kwa taarifa alizonazo, alisema mbegu ya mahindi aina ya tembo, katika baadhi ya maeneo inauzwa hadi Sh20,000, ilhali makubaliano yalikuwa isizidi kati ya Sh12,000 hadi Sh14,000. “Tulikubaliana na kampuni ya Seed Co kwamba bei isizidi hiyo, baada ya kutangazwa Oktoba 20, mwaka huu, hawatotakiwa kuuza zaidi ya bei hiyo na wanielewe kabisa nasema mbele ya mwenye nchi Rais wetu, sitasita kuwafutia leseni ya kuuza mbegu katika nchi hii,” alisema. Kwa kuwa kampuni hizo zimepewa ardhi na kuwekewa miundombinu ya kuzalisha mbegu, alisema wakienda kinyume na bei elekezi watashughulikiwa. Aliitaka kampuni ya Seed Co kuhakikisha inatoa bei elekezi hizo katika magazeti, huku Wakuu wa Wilaya wakipewa jukumu la kufuatilia madukani na iwapo zitauzwa kinyume wayafungie. Bei ya mahindi Katika mazungumzo yake hayo, Bashe alisema kuyumba kwa bei ya mahindi sokoni kunatokana na kufungwa kwa ununuzi wa bidhaa hiyo uliokuwa unafanywa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA). Alisema hadi sasa wakala huo umenunua mahindi yenye thamani ya Sh186 bilioni na imeshawalipa Sh143 bilioni, huku Sh43 bilioni zikitarajiwa kulipwa baada ya wiki moja. “Baada ya wiki moja Mikoa yote ya Kaskazini, Nyanda za Juu Kusini na kati ambayo ndiyo vilikuwa vituo vya kununulia wataanza kulipa, ilitufungue vituo vingine kwa sababu najua baada ya NFRA kufunga bei ya mahindi imeyumba,” alisema. Kauli hiyo ya Bashe, inajibu pia hoja ya Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo aliyoiibua hibi karibuni akisema katika ziara aliyoifanya kwenye Mkoa wa Rukwa, wakulima wengi waliilalamikia NFRA kutowalipa fedha zao. “Ninaiagiza wizara ya kilimo, wakulima waliouza mazao yao walipwe haraka, lakini kuna mahindi wanayo ndani wanahofia kuuza kwa kuwa NFRA wameondoka, naagiza wizara kwenda kuyanunua haraka,” alisema Chongolo. Kuhusu mahindi nje ya nchi Hata hivyo, Bashe aliwataka wakulima wasikatishwe tamaa na kauli iliyotolewa na moja ya nchi kuhusu kusitisha vibali vya kuagiza mahindi nje ya nchi. Oktoba 6, mwaka huu Rais wa Kenya, William Ruto alitangaza kusitisha vibali vya uagizaji wa mahindi na ngano kutoka nje ya nchi, akisema atabatilisha uamuzi wake huo pake nchi yake itakapokabiliwa na uhaba wa chakula. Kuhusu hilo, Bashe aliwasisitiza wakulima, “msiwe na wasiwasi Serikali ipo pamoja nanyi, wakifunga kwanza kwa mwaka huwa wananunua tani 400,000 tu, hizo Serikali ya Rais Samia haitashindwa kuzinunua,” alisema. Katika mazungumzo yake mbele ya wananchi hao, Bashe aliwahakikishia wakulima wa ngano nchini kwamba Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) itanunua tani zote 5,000 wilayani Hanang. “Pia nimezungumza na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) anunue ngano nyingine zote zilizopo kwenye maghala na hilo litafanyika baada ya wiki moja,” alisema. Katika ziara hiyo, Rais Samia alisisitiza umuhimu wa wakulima kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani kama msingi wa uuzaji wa mazao yao. Alisema hata kama zao halijaingizwa kwenye mfumo huo, halmashauri husika inayo nafasi ya kuliingiza iwapo itakubaliana na wakulima na kama limelimwa sana. Katika kauli yake hiyo, aliwataka viongozi mbalimbali kuacha kuweka vikwazo unapofika wakati wa mauzo ya mazao. “Kuna vikwazo mkulima hajui aende wapi, mazao yanadorora tujipende,” alisema. Akiwa mkoani Singida kwenye mikutano wa hadhara, Rais Samia aliwapongeza wananchi wa Mkoa huo kwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo, ikiwemo mbaazi, mahindi, alizeti na mengine. Kulingana na mkuu huyo wa nchi, hatua hiyo ni faraja kwake kwani inawezesha taifa kuwa na uhakika wa chakula. Kilichomfurahisha zaidi, alisema ni hatua ya Mkoa huo kutokuwa miongoni mwa ile inayokabiliwa na lishe duni kama ilivyo mingine inayozalisha zaidi. Katika mikutano huo, Mbunge wa Manyoni Mashariki, Pius Chaya aliibua changamoto ya umeme akisema katika eneo hilo hakuna kituo cha kupoozea nishati hiyo. Akijibu hilo, Rais Samia alisema Serikali ipo katika mpango wa kujenga kituo cha kupoozea umeme na Sh32 bilioni zimetengwa. Pamoja na hilo, alisema mradi wa umeme wa jua wa Sh80 milioni unatarajiwa kujengwa katika eneo hilo. Kadhalika, alisema Sh10 bilioni imetolewa na Serikali kulinda umeme usikatike mara kwa mara kama hatua za muda mfupi. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba alisema wakazi wa Manyoni kwa sasa wameamua kulima zao la Korosho na wanatarajia kuwa wazalishaji wakubwa baada ya miaka mitatu. “Korosho yetu ni ile iliyofanyiwa utafiti pale Naliendele kwa hiyo tutazalisha kwa mbegu bora,” alisema. Alieleza Mkoa huo una vijiji 441 na hadi Desemba mwaka huu jumla ya vijiji 401 vitakuwa tayari vimeshapelekea huduma ya umeme. “Desemba mwakani vijiji vyote vya Mkoa wa Singida vitakuwa na huduma ya maji safi na salama na tutaweza kwa sababu tuna mashine ya kuchimbia visima,” alisema.
Hatma ya uwanachama wa Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga ndani ya chama chake cha ADC upo katik
Hatma ya uwanachama wa Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga ndani ya chama chake cha ADC upo katika mashaka, kutokana na viongozi wake kudai kanuni za chama hicho zimemuondoa. Kulingana na viongozi hao wa ADC, kanuni za chama hicho zinabainisha uhalali wa mwanachama utatokana na ushiriki wake kwenye shughuli za chama hicho, jambo ambalo Sendiga hakulifanya kwa miaka kadhaa. Hata hivyo, mwenyewe ameweka wazi kuwa, hana muda wa kuzungumzia masuala yanayohusu chama, badala yake amejikita kutekeleza miradi mbalimbali kwa maendeleo ya wananchi wa Mkoa anaouongoza. Hayo yanajiri ikiwa ni miaka miwili tangu Sendiga ateuliwe na Serikali ya CCM, kuwa Mkuu wa Mkoa, akianzia Iringa Mei 25, mwaka 2021 na baadaye alihamishiwa Rukwa kisha Manyara alipo sasa. Ndani ya ADC, Queen hakuwa mwanachama tu, alikuwa kiongozi pia kwa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Bara na kupitia chama hicho mwaka 2020 aliwania nafasi ya urais. Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi jijini hapa, Naibu Katibu Mkuu wa ADC bara, Innocent Siriwa alisema kutoshiriki kwake katika shughuli za chama hicho kumeondoa uhalali wa uanachama wake. Siriwa aliyeukwaa wadhifa huo akichukua nafasi ya Queen, alieleza mwenendo wa kutoshiriki shughuli za chama hicho zilianza mara tu alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mei mwaka 2021. “Kuanzia hapo hakuonekana tena katika chama, hakushiriki shughuli yoyote iwe ya kikanuni au vinginevyo, kwa kufanya hivyo kwa mujibu wa Katiba yetu umejiondoa,” alisema. Hata hivyo, alisema wangetamani kuwa naye ndani ya chama hicho, lakini kwa vitendo vyake hivyo hawana budi kukubaliana na uhalisia. "Siasa inahitaji hiari sio kulazimisha, yeye ana umri zaidi ya miaka 18 na ana uhuru wake wa kufanya mambo binafsi. "Sisi tungetamani kuwa naye na tungependezwa sana lakini yeye anaonekana hatamani ndiyo maana haonekani," alisema. Hilo linapigiwa msumari na Naibu Katibu Mkuu wa jumuiya ya wanawake wa ADC, Farida Kongoi aliyesema Queen hakuwahi kutoa taarifa yoyote ya udhuru wa kutoshiriki kwake shughuli za chama. “Kama bado ni mwanachama hatakuwa mwanachama hai, kwa sababu hata ada za uanachama halipi, kimsingi amejiondoa kikanuni,” alisema. Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Queen alisema kwa sasa hayupo kwenye nafasi ya kuzungumzia masuala ya vyama, kwa kuwa yupo kwenye shughuli za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wake. “Kwa sasa siko kwenye nafasi ya kuongelea masuala ya vyama. Niko busy kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na huduma kwa wananchi wa mkoa wangu (Manyara),” alijibu Queen. Mtazamo wa kisomi Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe alisema kihistoria wapo wengi walioteuliwa kushika nafasi mbalimbali ndani ya Serikali na wakaamua kujiunga na CCM. Alieleza hilo linasababishwa na ukweli kwamba, inawawia vigumu kutumikia mabwana wawili kutokana na utaratibu uliopo. Mathalan, kwa nafasi ya Mkuu wa Mkoa, alisema anayeteuliwa moja kwa moja anakuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM ya Mkoa husika, anakuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wa Mkoa husika na nafasi nyingine. “Hii inakuja kutokana na ukweli kwamba ukishateuliwa unakwenda kutekeleza Ilani ya CCM, sasa ukiamua kuendelea kuwa mpinzani maana yake unakwenda kupingana na unachokifanya haiwezekani,” alisema. Si nafasi za kisiasa pekee, alisema hata kwenye nafasi za utendaji wengi wanajikuta wakivihama vyama vyao na kujiunga na CCM, Profesa Kitila Mkumbo akiwa mmoja wao. “Aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Maji akiwa mwanachama wa ACT Wazalendo akaachana na chama hicho akajiunga na CCM, kwa hiyo wengi wanaosema mimi mpinzani wakati ameteuliwa ni maneno tu, huwezi kujipinga mwenyewe,” alisema. Hata hivyo, alisema hakuna mwenye makosa katika suala hilo, akifafanua mamlaka ya uteuzi imepewa wajibu wa kikatiba kumteuwa yeyote inayemuona anafaa. Kwa mtazamo wake, Dk Kabobe alisema utaratibu huo hauko sawa na unapaswa kubadilika. “Tuifanye Katiba yetu iruhusu vyama kuungana ili kuondoa mtazamo kwamba upinzani ni uadui, ufike wakati kila mmoja kwa kuwa ni Mtanzania aonekane anastahili na anafaa, tukiweza hilo, tutaweza kuwa na Wakuu wa Mikoa kutoka vyama vya upinzani,” alisema. Katika siasa, mbali na kuwania urais kwa tiketi ya ADC, Queen amewahi kuwania ubunge wa Kawe kupitia chama hicho. Lakini kabla ya kuwa mwanachama wa ADC, mwanasiasa huyo alikuwa kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na alikihama chama hicho mwaka 2014. Hata hivyo, kumekuwa na mstari mwembamba wa mwanasiasa kutoka upinzani anapoteuliwa kuendelea kubaki na chama chake hasa katika wadhifa wa Mkuu wa Mkoa. Ilishuhudiwa kwa marehemu Anna Mghwira alipoteuliwa na Hayati John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro akiwa mwanachama wa ACT Wazalendo lakini baadaye alijiunga na CCM.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha ADC Bara, Innocent Siriwa amesema miongoni mwa mambo yanayokwamisha m
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha ADC Bara, Innocent Siriwa amesema miongoni mwa mambo yanayokwamisha maendeleo ya kisiasa ya vyama vya upinzani nchini ni ubinafsi wa vyenyewe kwa vyenyewe Kauli yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, kuna hali ya kuzibiana nafasi ya kufikia maendeleo kama yaliyofikiwa na vyama vingine vya upinzani hasa vyenye wabunge na madiwani. Siriwa aliyasema hayo katika mahojiano maalum aliyofanya katika ofisi za Gazeti hili, Tabata jijini Dar es Salaam. Alisema kama vyama vya upinzani vilipaswa kuungana katika mambo mengi, lakini bahati mbaya vinaishia kukejeliana na kupingana vyenyewe kwa vyenyewe. "Vyama vya upinzani vyenye wabunge na madiwani, vikao radhi kufunga vioo kwa wengine wasipate wabunge wala madiwani, kumekuwepo na makundi baina ya wapinzani hata kauli zinaashiria hilo," alisema. Alisema wapo viongozi wakuu wa baadhi ya vyama vya upinzani, wanaoviita vyama vingine vya upinzani kuwa ni vyama uchwara. "Ili twende sawa lazima tuungane, wapinzani wote tuonekane watoto wa Baba mmoja, kwa sasa tupo kama watoto wa Baba wa kambo," alisema. Kuhusu kushirikiana na CCM Alipoulizwa iwapo ADC inashirikiana na CCM, alikana akisema kuonekana kwao katika shughuli mbalimbali za Serikali ni kujifunza mambo yanavyokwenda nchini. Alieleza hata walipoomba kushirikishwa kwenye safari za mkuu wa nchi kwenda nje ya nchi, ni kutaka kujifunza kuhusu yanayoendelea nchini na watakapopata nafasi ya kuiongoza nchi wajue pa kuanzia. "Usipojifunza kuhusu miradi na mambo yanayoendelea nchini leo hii ADC ukashinda uchaguzi umejifunza lini, ndiyo maana tunakwenda hapa na pale tuone nchi ilivyo na mambo yanavyokwenda," alisema. Hata hivyo, alisema namna nzuri ya kuikosoa Serikali itatokana na kwanza kujua uhalisia wa makosa yake kwa kuyaona, ndiyo maana wamekuwa wakishiriki shughuli mbalimbali. Lakini, alisisitiza kuwa mpinzani haina maana ya upinga kila kitu, penye kosa utakosoa lakini penye mazuri lazima upongeze. "Sisi tunakosoa pale panapohitaji kukosolewa na tunapongeza panapohitaji kupongezwa, kwa sababu suala la kupongeza ni sehemu ya busara na hekima," alisema. Kulingana na Siriwa, chama hicho kilishawahi kutaka watu wapewe nafasi ya kujadiliana kuhusu mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uendelezaji Bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai. Hilo, alisema ni moja kati ya mambo mengi kilichowahi kuyakosoa ikiwemo kuhitaji Katiba Mpya, kanuni za sheria za uchaguzi na sheria ya vyama vya siasa. "Hayo yote tunakosoa lakini tukisema tunapongeza unasikika tu tunavyopongeza," alisema. Alipoulizwa msimamo wa chama hicho kuhusu Katiba, alisema kinahitaji mabadiliko ili ipatikane itakayokuwa rafiki kwa kila mtanzania. Hitaji lao hilo, alisema linatokana na ukweli kwamba chama hicho ni miongoni mwa waathirika wa Katiba na baadhi ya sheria hasa za uchaguzi. "Tumetoka kwenye uchaguzi tumeathirika, hata ule wa Mbarali mkoani mbaya tumeathirika, iweke leo sisi tuseme hatuhitaji Katiba Mpya, tunahitaji Kwa kuwa tunataka demokrasia ya kweli kwenye taifa," alisema. Alieleza ADC nacho kinapigania Katiba kwa kuwa wanachokihitaji ni kuona inapatikana ile itakayowezesha mazingira sawa ya siasa na sio kutegemea upande mmoja. Kuhusu Sendiga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga ni miongoni mwa wanasiasa walioteuliwa kushika wadhifa serikalini kutoka chama hicho. Siriwa alipoulizwa kuhusu mwanachama huyo, alisema kulingana na kanuni za ADC mwanasiasa huyo si miongoni mwao kwa kuwa amejiondoa kikanuni. "Tangu alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa hakuwahi kushiriki shughuli yoyote ya chama kwa hiyo ukifanya hivyo umejiengua," alisema. Hata hivyo, alisema wangetamani kuwa naye ndani ya chama hicho, lakini kwa vitendo vyake hivyo hawana budi kukubaliana na uhalisia. "Siasa inahitaji hiari sio kulazimisha, yeye ana umri zaidi ya miaka 18 na ana uhuru wake wa kufanya mambo binafsi. "Sisi tungetamani kuwa naye na tungependezwa sana lakini yeye anaonekana hatamani ndiyo maana haonekani," alisema. Mikutano ya hadhara Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake wa chama hicho, Farida Kongoi alisema pamoja na kufunguliwa kwa mikutano ya hadhara, inakiwia vigumu chama hicho kufanya mikutano hiyo kama ilivyo kwa vingine. Hilo linatokana na ukweli kwamba, uwezo wao wa kiuchumi ni mdogo zaidi ukilinganisha na vile ambavyo angalau vina wabunge na vinapokea ruzuku. "Mikutano ya hadhara inahitaji fedha, ndiyo maana tulikuwa tunapendekeza sana sisi wenye vyama visivyo na wabunge wala mdiiwani tupatiwe ruzuku ili kuendeleza shughuli zetu," alisema. Lakini, alisema hadi sasa tayari mikutano kadhaa imefanyika ikiwemo katika Mkoa wa Tanga. Uchaguzi wa ndani Farida alisema kuanzia Aprili hadi Mei mwakani, chama hicho kinatarajiwa kufanya uchaguzi wake wa ndani katika nafasi zote kuanzia chini hadi za kitaifa.
Naibu Waziri Mkuu, Dk Doto Biteko ametaka kutambuliwa kwa maeneo hatarishi yenye viashiria vya kuath
Naibu Waziri Mkuu, Dk Doto Biteko ametaka kutambuliwa kwa maeneo hatarishi yenye viashiria vya kuathirika na maafa yatakayotokana na mvua za Eli-Nino na uandaliwe mpango wa kuyakabili. Kauli hiyo ya Dk Biteko inakuja ikiwa ni miezi miwili tangu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Agosti 24, mwaka huu itangaze uwezekano wa kutokea kwa mvua za El-Nino nchini. Dk Biteko alitoa kauli hiyo jijini Dodoma jana, wakati akizindua mpango wa taifa wa dharura wa kuzuia na kukabiliana na madhara ya El Nino na kuukabidhi kwa mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na viongozi wa taasisi za Serikali. “Ni vema kuainisha na kuandaa rasilimali za kuzuia na kujiandaa kukabiliana na maafa yatakayotokea katika kila sekta, kuna haja ya kutambua maeneo yenye viashiria vya kuathirika na maafa na kuandaa mpango wa kuzuia madhara na kukabiliana nayo,” alisema. Dhamira ya mpango huo, kwa mujibu wa Dk Biteko ni kuhakikisha Serikaii, wadau na jamii inachukua hatua stahiki za kuzuia na kupunguza madhara yatakayosababishwa na mvua hizo. Hatua nyingine alizotaka zichukuliwe, alisema ni kuelimisha wananchi na kuwahimiza kuhama kutoka kwenye maeneo hatarishi. “Ni muhimu kuweka akiba ya chakula na kulima mazao yanayohitaji maji mengi pamoja na hatua za kuchukua tahadhari ili kuokoa maisha yao na mali,” alisema. Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini, alisema ni muhimu kutekelezwa mpango wa kuzuia milipuko ya magonjwa kwa binadamu, wanyama na mimea. Alizitaka mamlaka zinazohusika na mazingira kuhakikisha barabara zinapitika wakati wote, kuimarisha na kusafisha mitaro na makalavati, huku wanaohusika na maji, umeme na mawasiliano waweke mipango ya kuzuia madhara. Njia za majitaka ni miongoni mwa maeneo aliyotaka yasafishwe, huku akisisitiza usimamizi wa taka ngumu na uwepo wa maeneo ya kuzitupa. “Tuimarishe madaraja na kingo za mito na mabwawa katika maeneo yote ya kimkakati, tusimamie matumizi sahihi ya mitaro na njia za maji kwa kuzuia viwanda kutiririsha uchafu katika maeneo ya makazi na sehemu za kuzalishia maji. “Wizara, Idara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri zote ziandae mipango ya utekelezaji katika maeneo yao kwa kuzingatia mpango huu ulioandaliwa na kuhakikisha mvua hizi zinatumika kwa shughuli za maendeleo,” alisema. Aliitaka TMA iandae utaratibu wa kuwa inatoa taarifa za mwenendo wa mvua hizo kupitia ujumbe mfupi wa maandishi. Kadhalika, alizitaka wizara kutimiza wajibu wa kukutana na wadau kuwapa maelekezo mbalimbali, huku kwenye kila hotuba zao wahakikishe wanaelezea mvua hizo. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Jenista Mhagama alisema wizara hiyo imetekeleza na kuratibu hatua kadhaa za msingi na awali baada ya kutangazwa kwa mvua hizo. Miongoni mwa taarifa hizo, alisema ni kuwasilisha taarifa kwenye wizara na mikoa ili kufanya tathmini ya maeneo yanayoathirika na kuandaa mipango ya hatua za kuzuia au kupunguza madhara. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Ladislaus Chang’a alisema matukio kama hayo yataendelea kuongezeka kwa kadri joto la dunia linavyoendelea kuongezeka, kulingana na tathmini ya hivi karibuni. “Mwelekeo wa mvua za vuli kwa mwaka 2023 unaonesha msimu wa mvua za vuli utachagizwa na uwepo wa El Nino, tunaendelea kufanya kazi masaa 24 kufuatilia mabadiliko katika bahari zote. “Tunachokiona kwa sasa ni ukubwa wa El Nino kuwa katika nyuzi joto 1.2 ambao ni ukubwa wa wastani na tunatarajia mvua hizo zitaenda hadi Januari,” alisema.
Ili kurahisisha upatikanaji wa bima za magari, kampuni ya Bima ya Jubilee imetangaza kuanza kutoa hu
Ili kurahisisha upatikanaji wa bima za magari, kampuni ya Bima ya Jubilee imetangaza kuanza kutoa huduma katika vituo vya mafuta jijini Dar es Salaam. Imesema hatua hiyo itawaondolea wananchi usumbufu wa kufuata huduma hiyo katika matawi ya kampuni hiyo, badala yake watazipata pale watakapokwenda kuweka mafuta. Hayo yameelezwa leo, Oktoba 11, 2023 na Mkurugenzi wa Jubilee Allianz, Summit Gaurav wakati wa hafla ya makubaliano ya ushirikiano wa utoaji huduma kati ya kampuni hiyo na vituo vya mafuta vya Total Energies na Benki ya NBC. Amesema lengo la ushirikiano huo ni kusogeza karibu huduma za bima na kurahisisha upatikanaji wake. “Tunatarajia kufanya hivi nchi nzima kwa sasa tumeanza kutoa huduma za bima katika vituo vya mafuta vya Total Energies vya Dar es Salaam,” amesema. Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa Total Energies, Getrude Mbangile amesema huduma hizo zitapatikana katika vituo vitano jijini hapa. Amevitaja vituo hivyo ni Oyster bay, Morocco, Malimani City, Kariakoo na Samora. “Tunacholenga ni kuhakikisha tunatoa huduma jumuishi katika vituo vya mafuta, badala ya mafuta pekee mwananchi akija akutane na huduma nyingine,” amesema. Elibariki Kasuke kutoka NBC, amesema jukumu lao katika ushirikiano huo ni kuhakikisha wanamwezesha mteja ambaye hatakuwa na fedha ya inayotosheleza kupata huduma hiyo. “Kinachofanywa ni kulinda hasara inayosababishwa na ajali, tutatoa bima kubwa ambayo gharama yake itakuwa ni asilimia 3.5 ya gharama halisi ya gari husika, lakini tutatoa bima ndogo pia,” amesema. Amesema benki hiyo inatoa mikopo ya ada ya bima kwa ajili ya kumwezesha muhitaji kulipia bima na marejesho ni kuanzia miezi minne hadi 10.
Kama ulidhani kushamiri kwa teknolojia ya akili bandia (AI) kutazika kibarua chako, bado unayo nafas
Kama ulidhani kushamiri kwa teknolojia ya akili bandia (AI) kutazika kibarua chako, bado unayo nafasi ya kutumikia nafasi yako katikati ya ulimwengu huo wa maendeleo ya sayansi na teknolojia iwapo utazingatia. Mwananchi limezungumza na wataalamu mbalimbali wa teknolojia hiyo, wanaokupa mbinu za kulinda kibarua chako dhidi ya akili bandia inayoonekana kuingia kwa kasi duniani. Haja ya kuzungumza na watalaamu hao, imetokana na mitazamo ya wengi wakihofu kupoteza kazi, kwa dhana kuwa akili bandia itazifanya badala yao. Hofu hizo zinapata mashiko zaidi kutokana na tafiti mbalimbali duniani ukiwemo ule uliochapishwa Machi 26, mwaka huu na taasisi ya Goldman Sachs ya nchini Marekani unaoeleza, karibu theluthi mbili ya kazi Marekani na Ulaya kwa kiasi fulani zitafanywa na AI. Utafiti huo unakwenda mbali zaidi na kubainisha, teknolojia hiyo itafanya mageuzi ya kazi za kudumu milioni 300 duniani, kutoka kufanywa na watu hadi kufanywa kuotomatiki yaani na roboti. Kwa upande wa Tanzania, utafiti mdogo uliofanywa na taasisi binafsi ya ushauri wa masuala ya AI ya Sahara Ventures, umebainisha kati ya wasomi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) waliohojiwa, asilimia 57 walisema teknolojia hiyo itachukua kazi zao, huku asilimia 29 wakilipinga hilo. Utafiti huo uliohoji wasomi 60 wakiwemo wanafunzi, wahadhiri na wanataaluma wengine kutoka chuoni hapo, unasema asilimia 71 kati yao, waliona teknolojia hiyo italeta matokeo zaidi katika sekta ya afya, huku 14 pekee wakiitaja sekta ya kilimo, 10 wakitaja elimu na wengine watano walisema kwenye utawala. Kati ya wasomi hao waliohojiwa, asilimia 53 walisema ni bora kuhudumiwa na daktari binadamu badala ya roboti, huku 30 wakisema bora roboti na 17 walijibu hawana uhakika. Kwa upande wa viongozi wa siasa, asilimia 66 ya wasomi hao, walisema bora roboti zitumike kupanga mikakati ya nchi badala ya wanasiasa, huku asilimia 23 wakidhani wanasiasa wanafaa zaidi na 11 hawakuwa na uhakika. Kazi zilizopo hatarini Kama wewe ni mwalimu unapaswa kujiandaa, Shule ya kimataifa ya Indus nchini India mwaka 2019, imezindua roboti la kwanza linalofanya kazi ya kufundisha wanafunzi na mwaka 2027 ndiyo tekenolojia inayotarajiwa kutumika zaidi kwa usaidizi wa mwalimu kwa sehemu ndogo. Lakini, tayari hivi sasa kuna teknolojia ya Chat GPT, iliyozinduliwa mwaka jana, ikifanya kazi ya kuandika taarifa kwa kadri itakavyotakiwa kutoka katika vyanzo mbalimbali, unaweza kusema waandishi wa habari, waandishi wa machapisho, mawasilisho kazi zao kwa sehemu kubwa zinafanywa na teknolojia hiyo. Kulingana na Goldman Sachs, kwa kiasi kikubwa shughuli zenye mishahara ya kima cha chini na cha kati zitafanywa na teknolojia za akili bandia, huku zile kubwa ndizo zitakazofanywa na watu ambao kimsingi ni wachache wenye uwezo nazo. Unachopaswa kufanya Kuna haja ya kuwa na maarifa na uwezo wa ziada ili kumudu ushindani katika soko la ajira ndani ya zama za matumizi ya akili bandia, kama inavyoelezwa na Dk Zena Katima, mhadhiri kutoka idara ya uhandisi na teknolojia wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). "Mfano kwa wanafunzi, akili bandia itakusaidia kuandika ripoti na mambo mengine, lakini unahitaji kuwa na uwezo wa ziada wa kuiwasilisha ili ieleweke, hapo utakuwa na umuhimu," anasema. Kinyume na hivyo, anasema hautakuwa na nafasi katika eneo lolote kwa kuwa mambo ya kawaida unayofanya tayari teknolojia imekuja kuyafanya. Hata hivyo, anasema kuibuka kwa teknolojia hiyo kunaweza kuathiri vijana wengi, kwani inawasaidia kufanya walivyopaswa kuvifanya na bahati mbaya wanabweteka. Anaeleza namna pekee ya kuonyesha umuhimu wao ni kujiandaa kuwa na ziada juu ya kile kinachofanywa na akili bandia, ili hata mwajiri aone haja ya kuajiri kijana. "Huku vyuoni vijana ukiwapa kazi wanaotumia Chat GPT kupata majibu kisha wanakuletea, hii unawafanya wabweteke, hawafikirii maarifa ya ziada kuitangulia Chat GPT ili waendelee kuwa na umuhimu katika soko la ajira," anasema. Ili kulinda kibarua chako katika zama hizo, anasema ni muhimu kujiandaa kwa kuwa na maarifa ya ziada. Mkurugenzi wa Afya Intelligence, Harrison Mariki anasema kitakachomchukulia mtu ajira yake sio teknolojia hiyo, bali ni mtu mwingine anayeitumia. “IA ipo kwa ajili ya kurahisisha kazi na kuifanya kwa ufanisi akitokea mtu mwenye uwezo wa kuitumia vizuri atachukua kibarua chako, muhimu ni kujifunza kuendana nayo ili ikukute na uwezo wa kuitumia,” anasema.
Nguvu za wananchi wa Kijiji cha Hoyoyo wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani kujitolea katika ujenzi wa za
Nguvu za wananchi wa Kijiji cha Hoyoyo wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani kujitolea katika ujenzi wa zahanati na Kituo cha afya, hazikuwafaa kupata huduma za afya kijijini hapo. Hiyo ni kutokana na kukwama kwa hatua ya kuwekwa miundombinu ya huduma hizo na uzinduzi wa majengo hayo kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Mwandishi wa habari hii ameshuhudia majengo hayo yalivyogeuka nyumba za popo na wadudu yakizingirwa na mapori, huku baadhi ya miundombinu ikianza kuharibika kutokana na kutotumika kwa muda mrefu. Nyuma ya pazia la mkwamo huo, kulingana na wananchi ni mwenza wa Rais mstaafu, Salma Kikwete aliyefadhili ujenzi wa kituo hicho cha afya kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) ambayo yeye ni Mwenyekiti wake, lakini sasa imegeuka na kudai ni mali yake, kinyume na wananchi walivyoahidiwa wakati wa ufadhili huo. Kwa mujibu wa wananchi, wakati wa ufadhili wa ujenzi wa kituo hicho, Salma aliahidi baada ya majengo kukamilika angekabidhi kwa Serikali kuweka miundombinu iliyobaki na kuanza kutoa huduma, lakini ni miaka 10 imepita, bila utekelezaji wa ahadi hiyo. Alipotafutwa kwa simu kuzungumzia hilo baada ya kuulizwa swali, Salma simu yake ilikatwa na alipopigiwa tena mara kadhaa, iliita bila majibu. Hayo yanaendelea wakati wakazi wa Kijiji hicho wakitaabika kusafiri umbali wa kilometa saba hadi 10 kufuata huduma za afya. Wakizungumza na Mwananchi kijijini hapo, wananchi wanaeleza kuwepo hali isiyoeleweka juu ya mmiliki halali wa kituo hicho, kwani walitoa ardhi na nguvu zao kupata huduma, lakini sasa hawaelewi kinachoendelea. Wakati yote hayo yakiendelea, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija Nassir Ali anasema hana lolote la kusema hadi atakapofuatilia. "Siwezi kusema chochote hadi nitakapofuatilia," alijibu baada ya kuulizwa iwapo walishakabidhiwa na nani mmiliki halali wa kituo hicho cha afya. Ilianza hivi… Changamoto hiyo ilianza miaka 13 iliyopita, baada ya juhudi za wananchi, kujitolea kujenga Zahanati kwa ajili ya kusogeza karibu huduma za afya, kama anavyoeleza Pili Dengwa mkazi wa Kijiji hicho. Anasema baada ya vikao, mmoja wa wananchi, Shiriki Dengwa (Kaka yake) alijitolea eneo la ekari tatu kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati hiyo na mara moja michakato ikaanza kufanikisha hilo. "Wakati huo huduma ndiyo zilikuwa mbali zaidi ya sasa, ilikuwa kawaida wazazi kujifungulia nyumbani, ingawa sasa inafanyika hivyo lakini enzi hizo ilizidi," anasema. Kulingana na Pili, baada ya kupatikana kwa eneo, kila mwanakijiji alitakiwa kwenda kujitolea kulisafisha. Kwa kuwa ilikuwa shauku ya kila mmoja kuwa na huduma za afya kijijini hapo, Pili anasema shughuli ya usafishaji haikuwa shuruba kwao, hadi wanawake walijikuta wanang'oa visiki. "Wilaya wakati huo ilitusaidia baadhi ya vitu, lakini kwa sehemu kubwa wananchi ndiyo tulifanikisha ujenzi wa jengo la Zahanati katika eneo la ekari tatu," anasema. Mzee Dengwa aliyeshiriki kufyatua tofali za Zahanati hiyo ni Baba mzazi wa Pili, anasema ujenzi ulikamilika kipindi cha utawala wa Jakaya Kikwete. Tatizo lilianza baada ya ujenzi kukamilika, anasema alikuja mke wa Kikwete (Salma) na kutaka ajenge hospitali kubwa zaidi kwa kuwa iliyojengwa na wananchi isingekidhi mahitaji. Anasema Salma aliahidi kulitekeleza hilo kwa ufadhili wa Taasisi ya WAMA na kwa kuwa lilikuwa wazo chanya liliibua faraja zaidi kwa wananchi. Katika utekelezaji wa hilo, anasema Salma alinunua eneo kubwa na ndani yake akatoa ekari mbili zichanganywe na zile tatu za wananchi kufanikisha ujenzi huo. Kipindi hicho, anasema Salma alikuwa akienda mara kwa mara kukagua maendeleo ya ujenzi na ulipokamilika ndipo safari zake zilipokoma. "Huku ndiko alikokuwa anaishi Baba yake mzazi (Salma), sasa jengo lilipokamilika Baba yake alifariki, kuanzia hapo ndiyo ulikuwa mwisho wa kumuona yule mama," anasema. Kwa tathmini ya Dengwa na ushuhuda wa mwandishi wa habari hii, jengo hilo linakaribia hadhi ya kuwa Kituo cha Afya kinachotoa huduma zote muhimu za afya. Kinachokosekana kulingana na Dengwa, ni miundombinu ya kutolea huduma hizo vikiwemo vifaatiba, vitanda vya wagonjwa samani za ofisini na wahudumu. "Miundombinu mingine yote kama umeme na maji yapo kwani kilichimbwa kisima kirefu isipokuwa kwa sasa pampu imeibwa," anasema. Wakati kukiwa na matumaini ya upatikanaji wa huduma bora za afya tena kwenye jengo kubwa, anasema mambo yalianza kuharibika. Kuharibika kwake, kulitokana na kile alichoeleza, ahadi kadhaa za siku ya kuwekwa miundombinu na kuzinduliwa zilibaki hewa na kuwatumbukia nyongo wananchi. Matumaini ya wananchi kupata huduma za afya kijijini hapo, anasema yakaanza kupotea huku waliojitolea wakilalamikia nguvu zilizotumika bila mafanikio. Ilifika mbali zaidi, anasema hadi aliyetoa eneo la ekari tatu akaanza kudai alipwe, kwa kuwa dhamira ya kulitoa kwake haitimizwi. Si hayo tu, anasema lawama zikafika hadi kwa viongozi, wananchi wakitaka angalau eneo walilojenga kwa nguvu zao (Zahanati) lizinduliwe huduma zianze kutolewa, lakini yote hayo hayakuzaa matunda. Kulingana na Dengwa, danadana zilianza kati ya Serikali na Salma, kila mmoja akimtupia mpira mwenzake kuwa ndiye mwenye mamlaka ya kuendeleza palipoishia. "Serikali ya Wilaya ilitwambia jengo linamilikiwa na WAMA, huku mama (Salma) akitwambia imebaki Serikali kulizindua," anasema. Baada ya kulalamika kwa Serikali ya Kijiji, Dengwa anasema walitakiwa kuunda kamati kwenda Dodoma kumfuata Salma na hawakufanikiwa kuonana naye. Ziara kadhaa za viongozi wa Serikali, anasema zimefanyika katika majengo hayo bila matumaini yoyote ya kuzinduliwa. "Kwa sasa yamebaki kama magofu yamezingirwa na mapori, roho zinauma lakini hatuna cha kufanya," anasema. Si zahanati iliyojengwa kwa jasho la wananchi wala kituo cha afya kilichojengwa kwa ufadhili wa WAMA, Dengwa anasema vyote havijazinduliwa na sasa ni majengo tupu yaliyozingirwa na mapori. Tuhuma kwa Serikali Mwanakijiji mwingine ambaye hakutaka jina lake litajwe, anaituhumu Serikali akisema inafanya njama ya upigaji fedha. Tuhuma zake hizo, alizijenga kwa hoja kwamba, inawezekanaje Serikali iamue kuanza ujenzi wa Zahanati mpya ya Kijiji ilhali kuna majengo yaliyokamilika yanahitaji vifaa tu. "Wanataka wale, kwa sababu haya majengo hayakujengwa na wao kwa hiyo hawakupata ulaji, ndiyo maana wameanzisha ujenzi kule Kitongoji cha Gogo wanajua hela itapitia mikononi mwao," anasema. Alichojibu Mwenyekiti Lakini, hoja hiyo inajibiwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Suleimam Kurusule anayesema uamuzi wa ujenzi wa zahanati unaoendelea sasa, ulitokana na maelekezo kutoka halmashauri. Baada ya halmashauri kueleza hospitali iliyojengwa inamilikiwa na WAMA, anasema ilikishauri Kijiji kama kinahitaji zahanati kinapaswa kujenga ya kwake. Ushauri huo, anasema uliambatana na uamuzi wa halmashauri hiyo kutoa tofali 6,000 kwa ajili ya ujenzi na kilichofanywa naye ni kushirikiana na viongozi wenzake kusaka eneo la ujenzi. "Tulimtafuta mdau alitusaidia eneo la ekari mbili tukaanza ujenzi wa zahanati ambayo tangu halmashauri itoe tofali haikutoa fedha yoyote tunajenga kwa mapato ya Kijiji," anasema. Kwa sasa, anasema imefikia hatua ya kupauwa lakini bado ujenzi unagharimiwa kwa fedha za Kijiji na baadhi ya wadau na zaidi ya Sh30 milioni zimetumika. Kuhusu hospitali iliyokwama, anasema kwa kuwa wananchi walijitolea bila mafanikio, imekuwa vigumu kushawishika kujitolea tena katika zahanati inayojengwa sasa. "Kila kijana ukimwambia anakataa anakwambia tulishajitolea hatuoni umuhimu wake, kwa kweli imeturudisha nyuma," anasema. Hata hivyo, anasema aliingia madarakani mwaka 2019 na kila kikao hitaji la zahanati ilikuwa moja ya ajenda. Masafa kufuata huduma Itakupasa kusafiri umbali wa kilometa 10 kufuata huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kutokea Kijiji cha Hoyoyo, kama anavyoeleza Mariam Twaha mkazi wa eneo hilo. Mariam aliyekuwa Mjumbe wa Serikali ya Kijiji wakati wa ujenzi wa Zahanati ya awali, anasema umbali kutoka kilipo Kijiji na Hospitali hiyo umesababisha vifo kadhaa vya wananchi. "Watoto wakiumwa degedege hadi ufike hospitali, tayari wameshafariki tunapoteza watoto wengi sana siwezi kuhesabu," anasema. Kinachomshangaza, anasema ni hatua ya Serikali ya eneo hilo, kudai mamlaka ya hospitali hiyo ipo chini ya WAMA ilhali imejengwa kwenye ardhi iliyotolewa na wanakijiji. "Tunaambiwa haiwezi kufunguliwa kwa sababu ya WAMA, basi tumekaa ndo hivyo hivyo WAMA, WAMA, WAMA... hatujui wapi twende, tumekaa tu," anasema. Hali ya kutoaminiana Kilichotokea katika hospitali ya awali, kimezua hali ya kutoaminiana kati ya wananchi na viongozi wa Serikali ya Kijiji hicho kama anavyofafanua Mwenyekiti wa Kitongoji cha Gogo kilichopo katika Kijiji cha Hoyoyo, Rashid Malombwa Anasema danadana zilizopigwa zimesababisha wananchi kudhani viongozi wanawadanganya na wapo wanaodhani yanayotokea yana mkono wa Serikali ya Kijiji. Anaeleza hadi sasa jengo la zahanati ya awali lililositishwa na Salma Kikwete lina zaidi ya miaka 10 likiwa limekamilika bila kutumika. Kwa sasa, anasema huduma za afya wanafuata Mvuti wilayani Ilala Dar es Salaam au katika Hospitali ya Mkuranga mkoani humo, ambazo zote zipo mbali. Walikosea hapa… Diwani wa Tengelea kilipo kijiji hicho, Shabani Manda anasema kuna makosa yalifanyika wakati wa ufadhili huo ndiyo sababu unatokea mkwamo uliopo. Pamoja na sehemu ya ardhi kutolewa na wananchi, anasema umiliki wa eneo hilo kwa sasa unaonekana chini ya WAMA. Hilo, linatokana na kile anachoeleza, makubaliano ya ujenzi huo hayakufanyika kwa maandishi yalikuwa maneno mdomoni pekee. Kutokana na mazingira hayo, anasema kwa vyovyote majengo hayo yote mawili ni mali ya WAMA kulingana na nyaraka. Hilo linathibitishwa na kile alichoeleza, nyaraka za umiliki wa eneo zinaonyesha ni mali ya WAMA, hivyo hakuna kipengele kinachohalalisha wananchi, Kijiji wala Serikali kumiliki, ingawa Mwananchi halikuonyeshwa nyaraka hizo. "Ingekabidhiwa kwa Serikali ningeshajua maana mimi ndiye Diwani, lakini nina uhakika haikukabidhiwa kwa Serikali ni mali ya WAMA," anasema. Hilo, anasema linaifanya Serikali kukosa nguvu ya kushinikiza lolote, badala yake wamebaki kufanya juhudi za kwenda kumuomba Salma aridhie ifunguliwe, lakini hakuwahi kuwajibu. "Tulipoona mambo yamefikia huko, tukasema tusijicheleweshe ngoja tuendelee na utaratibu mwingine, ndiyo hapo tulipoamua kuanza ujenzi wa zahanati yetu unaoendelea sasa," anasema. Lakini, anasema kwa taarifa alizonazo, kuna wakati Salma alitaka kuunda ubia na Serikali kwa maana wagawane hisa za umiliki. Kilichokwamisha, anasema ni taratibu za sheria zinazotaka ushirikiano wa umiliki wa maeneo ya huduma za afya unapaswa kuanza na ngazi ya Kituo cha Afya. Kwa kuwa, jengo hilo halikuwa limekidhi hadhi ya kituo cha afya, anasema ilishindikana kuwa na umiliki wa pamoja. DC hajui lolote Alipoulizwa kueleza uhalisia wa umiliki wa zahanati hiyo na iwapo Serikali iliwahi kukabidhiwa, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija anasema hatakuwa na cha kuzungumza hadi atakapofuatilia. RC kuchunguza Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Aboubakar Kunenge anasema utata ulikuwepo kwenye umiliki wa zahanati hiyo kwa kuwa kuna Mwananchi aliyetoa eneo. Lakini, anasema kwa taarifa alizonazo kuna utata mwingine kwani ameelezwa kuwa Mwananchi huyo aliyetoa eneo baadaye aligeuka na kuamua kuliuza kwa Wama. “Tunafanya uthibitisho wa taarifa kama huyo mwananchi aliuza eneo kwa Wama na kama amefanya hivyo maana yake mwenye zahanati yake ni yule mwenye eneo, kwa maana aliyeuziwa ikiwa vinginevyo sawa,” alisema. Hata hivyo, alisema tayari ameshatuma timu ya watendaji kufuatilia hilo kwa ajili ya uthibitisho na hatimaye kupatikana suluhu ya utata uliopo. Aliyetoa eneo afunguka Shiriki Dengwa ndiye mwanakijiji aliyetoa eneo la ekari tatu kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati hiyo, anasema alilitoa bure eneo hilo na hakuwahi kuliuza kwa yeyote. “Nilitoa eneo kwa Kijiji tena kwa maandishi (amedai anazo nyaraka zote) kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji, nililitoa bure sikuuza,” anasema. Anaeleza yupo tayari kutoa ushahidi popote iwapo Serikali ya Kijiji itafungua madai ya umiliki wa Zahanati hiyo. “Inaniuma sana, nimetoa eneo kwa ajili ya jambo fulani hadi leo hakuna kinachoendelea, naona Serikali nayo imeamua kukaa kimya maana yule si unajua tena ni mke wa mheshimiwa,” anasema. Hii ndiyo Hoyoyo Ni mwaka wa 49 sasa tangu, Hoyoyo ipewe hadhi ya Kijiji mwaka 1974, hadi sasa hakina zahanati wala kituo cha afya. Ni miongoni mwa vijiji vya mwanzo baada ya uhuru wa Tanganyika kikigawanywa kutoka Kibugumo kwa Bwanabilatu enzi hizo. Tangu kuanzishwa kwake, wamepita wenyeviti sita na Kurusule wa sasa ni wa saba. Kabila la wazaramo ndilo hasa lenye asili na Kijiji hicho, kilichopakana na Mkoa wa Dar es Salaam katika pande mbili.
Hivi karibuni Rais Samia Suluhu Hassan alitangaza uamuzi wa kukiimarisha kitengo cha diplomasia ya u
Hivi karibuni Rais Samia Suluhu Hassan alitangaza uamuzi wa kukiimarisha kitengo cha diplomasia ya uchumi ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Nafahamu diplomasia ya uchumi ni miongoni mwa misamiati migumu kwa baadhi ya Watanzania, ingawa imekuwa ikisikika kutoka kwa viongozi mbalimbali. Tafsiri ya diplomasia ya uchumi, inatokana na linavyotafsiriwa neon diplomasia lenyewe. Kwa maana rahisi diplomasia ni mahusiano kati ya nchi moja na nyingine au shirika kutoka taifa moja na taifa lingine, au mahusiano ya shirika la nchi moja na Serikali ya nchi nyingine. Kwa hiyo unaposikia neno diplomasia maana yake ni mahusiano, isipokuwa yamegawanyika katika aina mbalimbali na kila aina ina maana yake, lakini leo tusiende huko ngoja tujikite kwenye diplomasia ya uchumi. Kwa maana hiyo ya neno diplomasia, tukija kwenye diplomasia ya uchumi, maana yake ni mahusiano hayo hayo lakini katika nyanja ya uchumi. Mahusiano katika nyanja ya uchumi yanahusisha vitu vyote ambavyo kimsingi vikifanyika matokeo yake yana maslahi ya kiuchumi baina ya mataifa yanayohusiana. Mathalan, ikifanyika biashara kati ya nchi moja na nyingine, matokeo yake ni uchumi, hivyo kitendo hicho ni utekelezaji wa diplomasia ya uchumi. Kwa hiyo inapozungumzwa diplomasia ya uchumi, maana yake ni mahusiano kati ya nchi moja na nyingine lakini katika masuala ya kiuchumi, biashara na mikakati mingine yenye maslahi ya kiuchumi. Kwa muktadha huo, hatua ya kuimarishwa kwa kitengo cha diplomasia ya uchumi, maana yake unawekwa mkazo wa kuhakikisha mahusiano ya Tanzania na nchi nyingine yanakuwa na maslahi ya kiuchumi. Diplomasia ya uchumi si jambo jipya na hata kitengo hicho kimekuwepo kitambo kidogo, tangu sera ya mambo ya nje ya mwaka 2001 enzi za Hayati Benjamin Mkapa ilipoweka mkazo katika diplomasia ya uchumi. Ingawa diplomasia ya uchumi ilikuwepo ndani ya sera hiyo na ulikuwa miongoni mwa misamiati iliyotajwa mara kadhaa na viongozi, utekelezwaji wake bado ulibaki kuwa changamoto. Balozi mbalimbali zinazoiwakilisha Tanzania nje ya nchi, ndizo hasa zenye jukumu kubwa la kuitekeleza dhana ya diplomasia ya uchumi, lakini kwa muda mrefu kulikuwa na kuchelea kwa mabadiliko hayo. Uhalisia ni kwamba balozi nyingi ziliishia kutekeleza majukumu ya kisiasa katika mataifa mbalimbali, badala ya kusaka fursa za kiuchumi kwa ajili ya Tanzania. Licha ya uwepo wa balozi mbalimbali katika mataifa tajiri duniani na yenye uhitaji wa bidhaa, wakulima nchini waliendelea kulalamikia masoko ya kuuza bidhaa zao za kilimo. Hayo yote ni matokeo ya kutotekelezwa kwa diplomasia ya uchumi ambayo pia inahusisha kusaka masoko ya bidhaa zinazozalishwa nchini ili kwenda kuuza katika nchi nyingine. Kama changamoto ilikuwa ni vigezo vya uzalishaji kukidhi mahitaji ya soko, nchi hizo pia zingetumika kuleta teknolojia nchini zitakazowezesha kukidhi vigezo hivyo na Mwisho wa siku soko lipatikane. Hatua ya kuimarishwa kwa kitengo hicho, ni kama inaamsha mitazamo ya balozi zetu kufikiri mbinu mpya za utendaji kutoka kupiga siasa hadi kusaka fursa kwa ajili ya Tanzania. Nafahamu wapo mabalozi ambao tayari wameshaendana na matakwa ya ulimwengu wa diplomasia ya sasa, sina sababu ya kumficha, Mbelwa Kairuki ni kielelezo sahihi, si peke yake wapo na wengine. Lakini, wapo ambao bado wanadhani kuwa balozi ni kuhakikisha mahusiano ya nchi yako na ile uliyopo hayaharibiki, kwa hivyo wanaishia kuonyesha uzuri na ukarimu wao, badala ya kuzisaka fursa pia. Kwa kuimarishwa kwa kitengo hicho, kinapaswa kuhakikisha kinabadili mitazamo ya utendaji wa balozi zetu, kila moja iwe chachu ya fursa za kiuchumi kwa nchi yetu, jambo litakaloliinua taifa. Kadhalika, kitengo hicho kihakikishe kinashauri maboresho ya kisheria na kisera juu ya mambo ambayo pengine ni kikwazo cha safari ya mageuzi ya utekelezwaji wa diplomasia. Hautafika wakati watanzania watalalamikia uhaba wa masoko wakati, wapo wawakilishi wa nchi kwenye masoko makubwa duniani. Haitatokea mtu akalalamikia teknolojia, wakati nchi ina mwakilishi katika taifa ambalo tayari limeshapiga hatua katika eneo ya teknolojia. Ni jukumu muhimu kwa balozi za nchi yetu kutekeleza diplomasia ya uchumi, huku diaspora wakitumika kama sehemu ya kiungo cha kulifanikisha hilo.
Licha ya unywaji pombe hufanywa kama sehemu ya starehe, kwa upande mwingine kuna machungu ndani ya k
Licha ya unywaji pombe hufanywa kama sehemu ya starehe, kwa upande mwingine kuna machungu ndani ya kiburudisho hicho kikihusishwa moja kwa moja na athari katika afya ya akili. Kulingana na wataalamu wa afya ya akili, pamoja na athari za afya ya mwili zitakazomkabili mtumiaji wa mvinyo kwa muda mrefu, mtu huyo yupo hatarini kuathirika kiakili pia. Tabia ya kinywaji hicho na namna kinavyofanya kazi katika mwili wa binadamu, ndicho kinachotengeneza tatizo katika akili, kama inavyofafanuliwa na Daktari Bingwa wa Saikolojia na Afya ya Akili, kutoka Hospitali ya Afya ya Akili Mirembe, Japheth Swai. Kwa mujibu wa Dk Swai, unapokunywa pombe pamoja na kupita katika maeneo mengine ya mwili, lakini uelekeo wake ni kwenye ubongo na kwenda kuuathiri. Na kwa kuwa akili inafanya kazi kwa kushirikiana na ubongo, anasema ukiathirika maana yake uhusiano wa akili na ubongo hautakuwa sawa. “Hapo sasa mtu atapoteza ule uwezo wake wa kufanya maamuzi kwa busara, kwa sababu pombe inakwenda kushambulia lile eneo ambalo lingetumika kutekeleza maamuzi ya busara,” anasema. Kama umefikia hatua ya kushindwa kufanya jambo fulani hadi upate ‘gambe’ basi juya tayari upo katika hali ya hatari ya afya yako ya akili, kulingana na Dk Swai. Anafafanua hatari zaidi inakuja pale ambapo pombe itatumika kwa muda mrefu, kwani inamfanya mtu aitegemee na kukosa uwezo wa kufanya lolote bila usaidizi wa kilevi hicho. “Mtu anaanza kuwa mtegemezi anakuwa hawezi kumudu lolote hadi atumie kilevi, ikishafikia hatua hiyo ndipo ambapo mtu awe amekunywa au hajanywa hawezi kuwa sawa sawa,” anasema. Kipindi hicho, anasema ndicho ambacho ugonjwa wa akili huanza kushamiri. “Unakuta mtu anakuwa tayari achukue fedha ya ada ya mwanawe akanunue pombe anywe, anakosa maamuzi ya busara hilo tayari ni tatizo la akili,” anasema. Hata hivyo, mtaalamu huyo anasema hatari ya pombe ni kubwa zaidi ukilinganisha na dawa nyingine za kulevya. Hilo linatokana na kile anachofafanua, pombe ndiyo mlango wa matumizi ya dawa nyingine zote za kulevya. Ni dawa ya kulevya Unapozungumzia dawa za kulevya nchini Tanzania, wengi watakuelewa ukitaja Bangi, Heroin, Cocaine na nyingine zilizoharamishwa kisheria, lakini kumbe pombe nayo ipo katika kundi hilo, kama Dk Swai anavyofafanua. Kinachotofautisha pombe na dawa nyingine za kulevya, anasema ni uhalali wa kisheria ilionao wa kutumika nchini, lakini nayo ni dawa ya kulevya. Kinachokifanya kinywaji hicho kuwa dawa ya kulevya, anasema ni tabia zake inapotumika katika mwili wa binadamu. "Pombe inalevya, pombe inavumbaza, pombe inakujengea uraibu na pombe inakufanya ufanye kitu kinyume na uhalisia wako, inakupa ujasiri wa uongo, hivi ni vitu vinavyofanywa na dawa za kulevya. “Dawa ya kulevya ni dawa yoyote utakayoitumia itakufanya uwe katika hali ya ulevi au kufanya ubongo wako usifanye kazi kama ilivyo kawaida,” anasema. Pombe na msongo wa mawazo Kile kinachotajwa kuwa pombe inapunguza mawazo ipo hivi, ukinywa kinywaji hicho utendaji wa baadhi ya viungo vyako vya mwili hupungua tofauti na uhalisia wake, kama inavyofafanuliwa na Dk Godwin Mwisomba mwanasaikolojia mwingine kutoka Hospitali ya Mirembe. "Kwa mfano ukiwa na mawazo kwa kawaida moyo unaenda mbio na hata shinikizo la damu linakuwa juu, sasa ukinywa pombe mapigo ya moyo yanapungua kabisa na hata shinikizo la damu linapungua," anasema. Hata ubongo, anasema unapokunywa pombe unapunguza uwezo wa kufikiri na hapo ndipo ambapo wengi huona mawazo yamepungua. Kawaida ya pombe, anasema unapokunywa inasababisha ubongo utoe homoni za furaha na ndizo zinazomfanya mtu ahisi vizuri baada ya kunywa. "Lakini homoni za furaha zinapatikana kwa njia ya kawaida, mfano ukiwa na kiu alafu ukanywa maji au ukiwa na njaa ukala chakula," anasema. Anaeleza ukitumia pombe kujipa furaha, unatengeneza njia bandia ya kutafuta furaha ilhali zipo njia za asili zinazopaswa kutumika. "Ukinywa pombe, ukivuta bangi unatengeneza njia bandia ya kujiletea furaha ilhali ipo njia asili," anasema. Hatari zaidi ni pale anaposema, kadri unavyokunywa pombe ubongo unajifunza kwamba furaha yako inatokana na kunywa na si vinginevyo. Kuanzia hapo, anasema mwili na ubongo unatengeneza tabia ya utegemezi wa pombe kama chanzo cha furaha na hapo ndipo uraibu huanzia. "Leo utakunywa moja itakupa furaha, kesho utakunywa moja itakupa furaha keshokutwa haitakupa itakutaka uongeze kiwango ili ikupe furaha hivyo hivyo hadi unafika wakati mtu anakunywa kreti nzima, hii ndiyo tabia ya pombe," anasema. Katika hatua hiyo, Dk Mwisomba anasema pombe inatengeneza mazingira ya kuudhibiti mwili, badala ya mtu kujidhibiti. "Uwezo wa kujisimamia unapungua, unafika wakati unakwenda baa kunywa chupa moja lakini unajikuta unakunywa zaidi, kwamba tayari pombe inakudhibiti wewe badala ya kujidhibiti au kuidhibiti, hii ndiyo tabia ya pombe," anasema. Ukifikia hatua hiyo, anasema mabadiliko ya tabia za mwili hutokea, kama uwezo wa asili wa kufanya kazi, kufikiri na mambo mengine hupungua. Katika hatua hiyo, anasema mwili na akili zote zinakuwa chini ya utawala wa pombe, badala ya yenyewe kutawaliwa na akili na mwili. "Hapo anakuwa na uraibu wa hali ya juu na madhara mengine ya mwili hutokea kwa sababu ukinywa pombe inavutwa na kuingiza kwenye mfumo wa damu," anasema. Anasisitiza tabia ya pombe katika mwili wa binadamu ni kuuvumbaza kwa maana huufanya ufanye kazi taratibu ukilinganisha na uhalisia wake. "Ukinywa pombe mapigo ya moyo yanapungua, shinikizo la damu linapungua, unaweza ukajisikia kulala,” anasema. Sio shida wanaokunywa kwa starehe Mhadhiri wa Saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Mabula Nkuba anasema pombe inasimama kama dalili ya changamoto katika afya ya akili ya mtu. Anaeleza wapo wanaokunywa pombe kama sehemu ya burudani kwao, akifafanua kundi hili hunywa kwa kiasi na unywaji wao haushinikizwi na jambo lolote. Hatari, anasema ni kwa wale wanaokunywa pombe kama sehemu ya kupunguza mawazo au kujisahaulisha matatizo waliyonayo wakati huo. “Pombe ukiitumia kawaida bila kushinikizwa na msongo, itabaki kama kinywaji ingawa ukiitumia kwa muda mrefu utapata madhara ya kiafya, lakini wanaoitumia kama kichaka cha msongo ndiyo wanaoathirika zaidi,” anasema. Hata hivyo, anasema anayetumia pombe kusaka furaha wakati wa huzuni anajulikana kwani, mara nyingi hujitenga hata anapokuwa baa. “Kawaida wanaokunywa pombe wanakuwa pamoja wananunuliana, lakini ukiona mtu amejitenda anakunywa akiwa peke yake, huwa ni wale walioshinikizwa na msongo,” anasema. Kulingana na Dk Nkuba, wenye msongo hujikuta wakitumia pombe zaidi ya kawaida kwa sababu ndiyo kitu wanachokifanya kama kisaidizi cha changamoto zao. “Ukifanya hivi inakufanya uitegemee na ikitengeneza utegemezi huo maana yake inatengeneza kitu kwamba bila pombe mtu hawezi kufanya kazi vizuri,” anasema. Hata ulevi wa kupindukia, anasema ni moja ya dalili ya matatizo katika afya ya akili. Mwenye msongo, anasema anaonekana anakunywa zaidi pombe si kwa sababu anaipenda ni kwa kuwa kuna msongo alioshindwa kuuhimili kwa nguvu zake na akachagua pombe kumsaidia. “Mara nyingi hawa ni watu ambao hawafunguki, hawaongei sana na hata ukiwakuta kwenye maeneo ya unywaji wanajitenga hawakai na wengine, hiyo ni dalili ya tatizo la afya ya akili,” anasema. Takwimu Takwimu zilizotolewa Oktoba mwaka huu na Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha wakati pombe ikikadiriwa kuuwa watu milioni tatu kila mwaka, watu wenye umri wa miaka 15 na kuendelea nchini Tanzania wanakunywa wastani wa lita 10.4, sawa na lita moja kila mwezi. Kuhusu matatizo ya afya ya akili, Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani (Unicef) linasema asilimia 20 ya vijana kote duniani wanakabiliwa na matatizo ya akili na kujiua ambayo ni sababu ya pili kuu ya vifo miongoni mwa vijana wa umri wa kati ya miaka 15- 19 kote ulimwenguni. Inakadiriwa mtoto mmoja kati ya sita walio na umri wa chini ya miaka 18 ana uwezekano wa kuwa na tatizo la afya ya akili hata hivyo asilimia 75 ya watu hao hawapati huduma zinazohitajika. Akisoma Hotuba ya Bajeti ya Afya kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alisema Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe katika kipindi cha Julai 2021 hadi Machi 2022 ilihudumia jumla ya wagonjwa 28,325 kati yao 26,761 ni wagonjwa wa akili wa nje (OPD) na wagonjwa wa akili wa ndani (IPD) 1,564. Aidha, wagonjwa wa msamaha waliopewa huduma walikuwa 3,985 ambao waliigharimu hospitali kiasi cha Sh60.2 milioni katika kipindi hicho. Jumla ya Wagonjwa 123, walipata huduma za kibingwa za saikolojia na wagonjwa 443 wa Neuro-psychiatry na wagonjwa wapatao 123 walifanyiwa uchunguzi na kuandikiwa taarifa za kisheria. Vilevile, katika kliniki ya afya ya akili kwa watoto na vijana wagonjwa 1,121 63 walihudumiwa. “Mirembe ilipokea wagonjwa wapya 225 wenye matatizo ya utumiaji wa dawa za kulevya na hivyo kufanya jumla ya waraibu wanaohudumiwa na kituo cha Itega kufikia 548 toka kilipoanza kutoa huduma mwaka 2020,” alisema Waziri Ummy. Dalili matatizo ya afya ya akili Mkuu wa Idara ya Afya na Magonjwa ya Akili Hospitali ya Bugando, Dk Catherine Magwiza anasema mtu kuhisi kukataliwa au kuwa na hatia na wakati mwingine kuhisi maisha yake hayana thamani ni dalili mojawapo kwani wakati mwingine anaweza kuwa na mawazo ya kutaka kujidhuru. “Mara nyingi tunasema mpaka condition iitwe ugonjwa lazima iwe imemsababishia kushindwa kufanya shughuli zake za kila siku, kushindwa kuhusiana na jamii yake, kuchangamana na watu na imemfanya amekosa utambuzi hivyo kuna hatua ikifika ndiyo tunasema ugonjwa wa akili,” anasema Dk Magwiza. Takwimu za Muhimbili zinaonyesha wanaume wakikabiliwa zaidi na tatizo hilo ikilinganishwa na wanawake kwa kipindi cha mwaka 2020/2021. Kati ya wagonjwa wa nje 24,014 walioonwa mwaka huu, wanaume walikuwa 15,205 ikilinganishwa na wanawake 8,809 ambao ni ongezeko la asilimia 17 ililinganishwa na wagonjwa 20,571 (wanaume 11,560, wanawake 9011) waliopewa huduma kwa kipindi kama hicho cha mwaka wa fedha 2019/2020. Sababu wanaume kuongoza Wataalamu wa afya ya akili na wanasaikolojia wataja sababu wanaume kuongoza kuwa ni pamoja na kuzongwa na majukumu, ugumu wa maisha, utafutaji, malezi, usiri, kukua kwa teknolojia, matarajio ya maisha, sonona, matukio ya nyuma na matumizi ya mihadarati na pombe kupindukia. Mtaalamu wa Afya ya Akili na Mwanasaikolojia kutoka Taasisi ya Mental Health Tanzania, Dk Philimina Scarion anasema wanaume hupata msongo wa mawazo ambao mwishowe hufikia sonona na kujikuta wakipata tatizo la afya ya akili. Anataja usiri kuwa sababu nyingine, “Dhana iliyojengeka miongoni mwa jamii ni kuwa mwanaume ni mtu mwenye nguvu, hivyo hapaswi kuonyesha udhaifu iwe ameumizwa kihisia na vinginevyo hivyo wanabaki kuwa wasiri, wanajiuliza maswali na kujijibu wenyewe, mwishowe wanachanganyikiwa,” anasema Dk Philimina. Anasema wengi hudhani anapoomba msaada wa mawazo au kuweka hisia zake wazi ni kuonyesha udhaifu tofauti na wanawake, wengi wao huongea na marafiki au kupiga umbea hii inawasaidia mno. “Wengine wanaathirika na matukio ya nyuma aliyoyafanya hawezi kuongea na mkewe, wengi mwishowe huchanganyikiwa,” alisema. Mtaalamu wa saikolojia, Dk Saldin Kimangale anasema ongezeko la wanaume pia linakuzwa na matumizi ya dawa za kulevya na ulevi kupindukia, “Hilo linachochea wao kupata magonjwa ya matumizi ya dawa za kulevya ambapo pia huchochea kupata magonjwa mengine kama Bipolar, Schizophrenia na magonjwa ya wasiwasi.” Mtaalamu wa saikolojia Josephine Tesha anasema, “Tusiwaambie watoto wa kiume ‘Jikaze Wewe ni Mwanaume’ wanaiweka akilini na ina athari kwao baadaye.” Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na Mkuu wa Kitengo cha magonjwa ya afya ya akili, Dk Frank Massao anasema, “Mara nyingi wanaume wanakumbwa zaidi na tatizo la afya ya akili kuliko wanawake, lakini pia kuna ongezeko kubwa la kasi ya maradhi ya akili.” Usuli Dalili 10 tatizo la afya ya akili - Kukosa usingizi au kulala kupita kiasi na mara nyingi mwathirika hukosa usingizi na kutafuta mbinu zingine ikiwemo vilevi. - Kukosa hamu ya kula au kula kupitiliza ambayo huchangia kwenye mabadiliko ya uzito wake kwa kuongezeka zaidi au kupungua sana. - Wivu uliopitiliza, kwa mujibu wa mwanasaikolojia na mshauri wa uhusiano, Deogratius Sukambi anasema wastani wa kesi saba kati ya 10 zinazofika ofisini kwake zinazohusu migogoro ya uhusiano na ndoa, zina uhusiano wa moja kwa moja na mmoja wao kuwa na dalili za tatizo la afya ya akili. - Hofu na wasiwasi uliozidi. - Hasira zilizozidi na ukali - Kuhisi kufuatiliwa na watu, kuona vitu ambavyo wengine hawavioni, kusikia sauti ambazo watu wengine hawazisikii au kuhisi mawazo yako yanajulikana au kutumiwa na watu wengine. - Mtoto kujitenga na wenzake au kuwa mtundu kupita kiasi, anapiga wanyama au wenzake, kukojoa kitandani zaidi ya miaka saba. - Kutopenda kufanya kazi, kama ni mfanyakazi hawezi kufanya majukumu yake vizuri, wapo ni mwanafunzi huanza kushuka kitaaluma na kama ni mama wa nyumbani lakini hawezi kufanya shughuli zake inavyotakiwa. - Kuacha kuongea na watu/kujitenga, furaha iliyozidi au huzuni kupita kiasi. - Kujikweza, kujiona mtu mkuu, mwenye uwezo wa kipekee au kitofauti kuliko watu wengine.
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), limesema hakuna kiongozi wa Serikali aliyewahi kutumia ndege za sh
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), limesema hakuna kiongozi wa Serikali aliyewahi kutumia ndege za shirika hilo kwenda ama ndani au nje ya nchi bila kulipia. Limesema safari zote za viongozi zinazoshuhudiwa wakitumia ndege za shirika hilo, huwa wanazikodi na kulipia gharama kama ilivyo kwa wateja wengine. Hayo yanaibuka kipindi ambacho, kumekuwepo na ukosoaji wa matumizi ya ndege hizo kwa viongozi wa Serikali, wananchi wakidhani zinatumika bure. Malalamiko dhidi ya matumizi hayo, yamekwenda mbali zaidi hadi kuhusishwa na sababu za kuahirishwa na kucheleweshwa kwa safari za ndege za shirika hilo. “Safari zinaahirishwa ratiba hazieleweki kwa sababu ndege wanapewa viongozi wanaenda nazo nje bure, badala ya kuziacha zifanye biashara,” amesema Denis Don mkazi wa Dar es Salaam. Akizungumza na Mwananchi Digital leo, Oktoba 4, 2023 Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi amesema kila inapoonekana ndege ya shirika hilo imetumika na kiongozi kwa safari ama za ndani au nje ya nchi, sio kwamba amepewa bure, bali anaikodi na kulipia gharama. Kulingana na Mhandisi Matindi, tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo ndani ya ATCL hakuwahi kutokea kiongozi aliyesafiri kwa ndege hizo bure, wote wanalipia ama kwa kukodi au kama abiria. “Watu wanafirikiri viongozi wanachukua ndege bure, hajawahi kutokea kiongozi aliyesafiri bure na haitatokea kwa sababu wamenipa shirika ili nizalishe, nipo tayari kuweka rehani nafasi yangu kama kuna kiongozi aliwahi kusafiri bure,” amesema. Ameusisitiza ufafanuzi huo kwa kile alichoeleza, Ofisi ya Rais ndiye mteja mkubwa wa kukodi ndege hizo, Kadhalika ndiye mlipaji mzuri, ingawa wapo wengine pia. “Huwa tunatoa muda wa kulipia, ukifika mimi mwenyewe nafunga safari nakwenda namwambia kwamba kuna deni kiasi fulani na linalipwa, haikuwahi kutokea haijalipiwa,” amesema. Hata hivyo, amesema upo utaratibu iwapo kiongozi atataka kukodi ndege, ikiwemo kutoa taarifa mapema ili kujua ratiba na kwamba imewahi kutokea mara kadhaa wamekosa. “Mbona imewahi kutokea mara kadhaa viongozi wanataka kukodi ndege tunawaambia kwa wiki hii ratiba imebana na hakuna aliyewahi kubisha au kulazimisha akodishiwe huwa wanaelewa,” amesema. Kuchelewa, kuahirishwa safari Kuhusu kuchelewa na kuahirishwa kwa safari za ndege hizo, Mhandisi Matindi amesema zipo sababu za ndani na nje ya uwezo wa shirika hilo, zinazofanya safari kuahirishwa. Amezitaja sababu zilizo nje ya uwezo wa ATCL ni kama hali ya viwanja, hali ya hewa, uwepo wa ndege maalum zinazopita katika anga na maelekezo ya waongoza ndege. Kwa upande wa zile zilizopo ndani ya uwezo wa shirika hilo, Matindi amesema ni hitilafu ya ndege, lakini inashindikana kutatuliwa kutokana na kutokuwepo mbadala. "Inapotokea ndege imeharibika au inahitilafu, lazima muwe na ndege mbadala, lakini uwezo huo bado hatujaupata kwa sasa,” amesema. Kulingana na uwezo wa sasa, Mhandisi Matindi amesema kinachofanyika ni kusubiri itengenezwe iliyopo na itaruhusiwa kuruka iwapo watajiridhisha na usalama wake. Lakini, ameeleza kwa kadri Serikali inavyoliongezea uwezo shirika hilo, ndivyo litakavyopunguza changamoto hizo. “Tunapaswa kuwa na ndege nyingi zaidi ili kudhibiti changamoto kama hizi, tunashukuru Serikali inatuwezesha, hii ni hatua nzuri, imetuongezea ndege, japo haitoshi kumaliza tatizo lakini inavyoendelea kufanya hivyo utafika wakati tutakuwa vema,” amesema. Amesisitiza, “bado shirika linajengwa, hatuwezi kusema sisi tupo kama wengine walioendelea, lakini Serikali inazidi kutuongezea uwezo.”
Changamoto katika utaratibu wa urasimishaji ardhi, zimetajwa kuwa chachu ya kukithiri kwa migogoro y
Changamoto katika utaratibu wa urasimishaji ardhi, zimetajwa kuwa chachu ya kukithiri kwa migogoro ya ardhi katika Jiji la Dar es Salaam, huku Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa akitoa siku saba za kutafutwa jawabu. Malalamiko juu ya changamoto za urasimishaji, yameibuliwa na viongozi mbalimbali katika Jiji hilo, wakisema kampuni binafsi zilizopewa kazi hiyo zimeishia kutoza fedha wananchi bila kuifanya kazi hiyo na kutokomea kusikojulikana. Mbunge wa Segerea, Bona Kamoli alisema, “Katika Jimbo langu, kampuni binafsi ya urasimishaji imekusanya fedha kwa wananchi bila kutekeleza kazi hiyo, hawa watu watafutwe warudishie fedha za watu au waje kutekeleza kazi waliyopaswa kuifanya,” alisema. Malalamiko kama hayo, yaliibuliwa pia na Diwani wa Kivule, Nyansika Getama aliyesema suala hilo limegeuka janga katika Kata hiyo, kwani pamoja na wananchi kutozwa fedha, kazi haikufanyika hadi sasa. Lakini, Getama aliibua na migogoro mwingine wa ardhi unaohusisha mipaka, ukiwemo wa Kisarawe na Ilala, Kadhalika Ubungo na Ilala. Mwenyekiti wa CCM Dar es Salaam, Abbas Mtemvu naye alikazia hoja hizo akitaja kukithiri kwa migogoro ya ardhi katika Jiji hilo, akisema kati ya Kata 102 za Jiji hilo, 80 walizotembelea wamekutana na malalamiko ya migogoro ya ardhi. Siku saba Akizungumza katika mikutano huo, kati ya watendaji wa wizara ya ardhi na viongozi wa CCM katika Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam jana, Silaa alitoa siku saba kwa Naibu Katibu Mkuu wake, Lucy Kabyemela kutafuta jawabu la changamoto za urasimishaji. Alitaka Kabyemela alitekeleze hilo kwa kushirikiana na watendaji wengine wa wizara hiyo na baada ya siku hizo, wakutane na viongozi hao kutoa mrejesho. “Kama kuna kampuni zimefanya vibaya tupate taarifa kwa ajili ya hatua na kwa kuwa haha tumeyazungumza hadharani basi wakati wa kutoa taarifa baada ya siku saba, tutatoa hadharani," alisema. Katika maelekezo yake hayo, Silaa alitaka majina ya kampuni binafsi za urasimishaji zinazolalamikiwa lakini hatua dhidi yao, ikiwemo kurudisha fedha. Katika kutafuta suluhu ya hilo, alisema maeneo yatakayohitaji fedha, watendaji wanapaswa kuyabainisha ili ziombwe au kutafuta namna ya kujibana ndani ya wizara ili zipatikane. Kuhusu kero ya urasimishaji, alisema kati ya simu 10 anazopokea saba zinalenga eneo hilo. Hata hivyo, alisema mkakati wa sasa wa Serikali ni kuhakikisha kunakuwa na Mkoa wa Ardhi katika kila Wilaya ya Mkoa wa Dar es Salaam. Hilo, alisema linalenga kusogeza karibu huduma za ardhi na wananchi kwa kuwa kumekuwa na mahitaji yasiyoendana na idadi ya watumishi. Mathalan, kwenye utoaji hati alisema kwa mwaka ofisi zilizopo Dar es Salaam zina uwezo wa kutoa 16,000 kwa mwaka, lakini ni chini ya zinazohitajika ingawa hakuzibainisha. Kulingana na Silaa, katika Jiji hilo ardhi yote ya kupanga na kupima imekwisha kutokana na idadi ya watu na kwamba maeneo mengi hayakupimwa wala kupangwa. Kutokana na hilo, alisema Serikali iliandaa utaratibu wa kuanzisha urasimishaji na kwa kuwa haikuwa na watumishi wa kutosha ikaingia makubaliano na kampuni binafsi. Huduma kusogezwa karibu Hata hivyo, Silaa alisema kwa sasa Serikali inatarajia kusogeza huduma za ardhi karibu na wananchi kwa kuifanya kila Wilaya ya Mkoa wa Dar es Salaam kuwa na Mkoa wa ardhi. “Huko nyuma Serikali ilikuwa na Kamishna wa Ardhi mmoja kwa ajili ya kutoa hati na baadae ofisi za Kanda, lakini sasa tunataka kuwa na Ofisi za Mkoa za Ardhi katika kila Wilaya ya Jiji la Dar es Salaam,” alisema. Awali, akifungua mkutano huo, Mtemvu alisema wingi wa migogoro ya ardhi katika Jiji hilo, ndiyo sababu ya kuitwa kwa waziri huyo. Hata hivyo, alisema migogoro yote inayohusiana na CCM, itawasilishwa kwa Katibu Mkuu, Daniel Chongolo atakayewasiliana moja kwa moja na Silaa.
Uteuzi wa Jokate Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) umetajwa kuibua damu c
Uteuzi wa Jokate Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) umetajwa kuibua damu changa ndani ya jumuiya hiyo. Hilo linatokana na ukweli kwamba, Jokate ndiye anayeonekana kuwa Katibu Mkuu kijana zaidi kuteuliwa katika wadhifa huo alioukwaa akiwa na umri wa miaka 36. Kauli kuhusu ingizo hilo la vijana, imeibuliwa na wasomi, kutokana na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kumteuwa Jokate Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa UWT. Kulingana na taarifa iliyotiwa saini na Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema, pamoja na Jokate mwingine aliyeteuliwa ni Raphael Lulandala kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM). Damu changa Akizungumzia uteuzi huo jana, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe alisema kiongozi huyo umeibua damu changa ndani ya jumuiya hiyo. Hata hivyo, alisema kilichofanyika ni ishara ya umakini wa chama husika, kwa kuwa chama makini lazima kitumie vijana wenye uwezo wa kukijenga. Ingizo hilo la vijana, alilitafsiri kama kete muhimu kwa CCM kutumia jumuiya yake ya UWT kujipanga vizuri zaidi kwenye chaguzi zijazo. "Kumbuka takwimu za uchaguzi zimeonesha kuwa wanawake ndio kundi kubwa hapa nchini na ndo wanaongoza kupiga kura ukilinganisha na makundi mengine. Kwa ufupi naweza kusema ukifanikiwa kushawishi wanawake kisiasa tayari unakuwa umeweka mtaji mkubwa sana. "Jokate ni kijana mwenye uwezo ana anaushawishi kwa vijana achilia mbali wanawake ambako nako pia anaweza," alisema. Kuhusu uwezo wake, alisema ni chaguo sahihi kwa Jumuiya hiyo na CCM kwa ujumla. "Kwa kipindi ambacho amekuwa Mkuu wa Wilaya ameonesha ukaribu wake na jamii hasa ya wanawake na jamii hiyo imemkubali sana," alisema. Alisema anachopaswa kufanya ni kujipanga kukabiliana na wapinzani wake kutoka vyama vingine. "Kwa mtazamo wangu haitakuwa rahisi maana najua vyama pinzani navyo mara nyingi vimekuwa vikiteua kujibu mapigo kitu ambacho kisiasa ni kizuri," alisema. Wadau washauri Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (Sauti), Dk Kanaeli Kaale alisema uteuzi na kupanda ngazi kwa Jokate katika nafasi mbalimba ni ujumbe kwa vijana wasomi na makada wa vyama vya siasa kuwa utendaji, uwajibikaji, kujituma, kujifunza na nidhamu kazini ni siri kufikia malengo na mafanikio katika nyanja zote. "Baadhi ya vijana wasomi na makada wanajibweteka walidhani usomi na ukada unatosha.....hapana! Pamoja na vyote, watu hupimwa kwa utendaji na nidhamu yao kazini," alisema Kaale ambaye pia ni mwandishi wa habari kitaaluma. Alisema akiwa Kisarawe, Jokate alidhihirisha uwezo wake katika kusimamia masuala ya msingi ikiwemo la elimu kwa watoto wa kike na hata alivyohamishiwa Korogwe alionyesha njia kwa kuhamasisha maendeleo, hasa kupitia vikundi vya ujasiriamali vya wanawake na vijana. Edwin Soko, mchambuzi wa masuala ya kisiasa aliunga mkono hoja hiyo huku akionya kuwa safari hii, Jokate anakabiliwa na mtihani mgumu wa kuonyesha uwezo wake kiutendaji na kiuongozi kutokana na siasa za ndani na nje ya Jumuiya za vyama vya siasa. "Jumuiya za UWT na UVCCM ni injini za CCM katika harakati za siasa kutokana na wingi wa wanachama wake....macho siyo tu ya CCM kama taasisi, bali pia hata makada wenye nia ya kuwania nafasi za uongozi yako kwa UWT na UVCCM," alisema Soko Alisema ugumu wa jukumu linalomkabili Jokate na mwezake unaongezwa na chaguzi zijazo za Serikali ya Mitaa mwaka 2014 na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Siasa ndani ya UWT na UVCCM Jokate na wenzake wanakabidhiwa dhamana ya kuwa watendaji wakuu ndani ya Jumuiya za UWT na UVCCM wakati kukiwa kumesalia muda mfupi Taifa kuingia kwenye chaguzi muhimu kuanzia Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu. Ingawa haitarajiwi hali na nguvu ya Jumuiya hizo kurejea zilipokuwa kabla na miaka ya mwanzoni mwa tisini, bado macho ya viongozi wa CCM yapo kwa viongozi na wanachama wa Jumuiya hizo linapowadia nyakati za uchunguzi. Wakati vijana kupitia UVCCM wanategemewa kwenye harakati na shughuli za kisiasa ikiwemo kampeni zinazohitaji matumizi ya nguvu, wanawake kupitia UWT wanalengwa siyo tu kwa wingi wao, bali pia utiifu wao kwa chama licha ya mawimbi ya kisiasa na kiuchumi wanayokumbana nayo. Uimara wa UWT na UVCCM kipindi cha nyuma kiliwalazimisha makada wa CCM wenye nia ya kuwania nafasi za uongozi ndani na nje ya chama kutafuta uugwaji mkono kutoka kwa viongozi na wanachama wa Jumuiya hizo kabla na hata baada ya chaguzi. Miongoni mwa viongozi waliovuma na kupata umaarufu wakati wakiongoza Jumuiya hizo ni pamoja na Dk Emmanuel Nchimbi aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Anna Abdallah na Sophia Simba waliokuwa wenyeviti wa UWT kwa nyakati tofauti. Harakati za kisiasa Jokate, Lulandala Wateule wote wawili hajawa na safari fupi katika harakati za kisiasa ambapo safari ya Jokate ndani ya CCM ilianza mwaka 2017 alipoteuliwa kuongoza Idara ya Uhamasishaji ya UVCCM akiwa na wadhifa wa katibu wa kamati. Mwaka mmoja baadaye, nyota ya mlimbwende huyo iliendelea kung'aa kwa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati John Magufuli kumteuwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani alikosimamia kwa juhudi haki sawa ya elimu kwa watoto wa kike na kiume. Baadaye alihamishwa kituo cha kazi kwa kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, kabla ya kupelekwa Korogwe mkoani Tanga kwa wadhifa huo hadi alipoteuliwa Jana kuwa mtendaji mkuu wa UWT. Katika eneo la ulimbwende, Jokate alishiriki na kushika nafasi ya pili katika mashindano ya kumsaka mlimbwende wa Tanzania mwaka 2006. Ushiriki wa mashindano ya ulimwende ulimfungulia njia katika shughuli mbalimbali ikiwemo a sanaa ya muziki na uigizaji. Kwa upande wake, historia ya safari ya kisiasa ya Lulandala inahudisha harakati na siasa za vyama vya upinzani ikiwemo kuwa miongoni mwa makada na viongozi waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Njombe. Mwaka 2015, Lulandala alikuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Njombe ambako pia amewahi kuwania kiti cha ubunge jimbo la Njombe Kusini kupitia tiketi ya chama hicho kikuu cha upinzani. Wakati wimbi la wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani kuhamia CCM lililobatizwa jina la kuunga mkono juhudi za aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Hayati John Magufuli, Lulandala alikuwa miongoni mwa makada wa Chadema aliojiunga CCM kabla ya kukwaa uteuzi wa kuwa DC na sasa kupewa uongozi wa juu wa Jumuiya ya UVCCM.
Mwenza wa Baba wa Taifa, Maria Nyerere amesema mtazamo kuwa kundi fulani limepitwa na wakati ni mion
Mwenza wa Baba wa Taifa, Maria Nyerere amesema mtazamo kuwa kundi fulani limepitwa na wakati ni miongoni mwa mambo yaliyolirudisha nyuma taifa. Maria ameihusianisha hoja yake hiyo na mtindo wa maisha wa zamani, akisema wazee na vijana walikutana kujadili mambo mbalimbali ya nchi. Maria aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana, alipotoa salamu katika uzinduzi wa msafara wa waendesha baiskeli 100 kwenda Butiama mkoani Mara, kuelekea kumbukizi ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere. Katika kauli yake hiyo, alisema kumekuwa na mitazamo kuwa kundi la rika fulani limepitwa na wakati, jambo ambalo limeirudisha nyuma Tanzania. "Kipindi kile cha mapungufu kijana na watu wazima walikuwa wanasikilizana kale ka misamiati ka amepitwa na wakati nako kameturudisha nyuma kidogo," alisema. Aliisisitiza hoja yake hiyo kwa mfano wa maisha ya zamani, akisema wazee na vijana walikutana kwenye maeneo ya michezo kujadili masuala ya nchi. Hata hivyo, hoja hiyo iliungwa mkono na Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Mohammed Bakary aliyesema kwa mfumo wa siasa za Tanzania hakuna aliyepitwa na wakati. Profesa Bakary alisema historia inaonyesha mataifa yote duniani yamejengwa kwa mchango wa watu wa marika yote yaani wazee na vijana. "Ikitokea vijana wamewaweka wazee pembeni kuna hatari na vivyo hivyo wazee wakiwaweka kando vijana," alisema. Hata hivyo, alieleza mfumo wa siasa za Tanzania ni vyama vingi ndani ya chama kimoja, ambao kimsingi umeasisiwa na wazee. Kwa sababu hiyo, alisema bado wazee wana nguvu katika kushauri uendeshwaji wa mfumo huo. "Wazee wana nafasi kubwa kwa kuwa ni mfumo waliouanzisha kwa hiyo kwa Tanzania mimi naona nafasi ya vijana ni ndogo zaidi kuliko ya wazee, hivyo ukisema wazee wamepitwa na wakati au ukiwaacha inaharibu," alisema. Katika hatua nyingine, Maria alisema kuna haja ya kufikiria namna ya kuhakikisha juhudi zinazofanyika ikiwemo msafara kama huo wa baiskeli zinaogezeka. "Mtumie safari hii kujifunza, kila Wizara inapaswa kuunda kikundi kikubwa kufanya shughuli kama hizi, lakini kifanye kulingana na mazingira ya sasa kama ni baiskeli, Pikipiki," alisema. Alisema kinachofanyika ni michezo na kwamba wengi wanafaidika kupitia hiyo. Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom Foundation Tanzania, Harriett Rwakatare alisema utunzaji wa mazingira, afya na elimu ni maono ya taasisi hiyo na ndiyo sababu iliyochagiza idhamini safari hiyo. "Pamoja na kwamba hili ni kama zoezi, lakini lina maana nzuri na linatoa taarifa nzuri kwa wananchi wengine," alisema. Alisema mbali na wanaoenda safari hiyo, wananchi wengine wanayo nafasi ya kuchangia madawati au miche ya miti kwa kutuma kiasi chochote cha fedha kuunga mkono kumbukizi hizo. Kuhusu msafara huo, Mwenyekiti wa Twende Butiama, Gabriel Landa alisema jumla ya waendesha baiskeli 100 wanameanza safari hiyo kuelekea Mutongo, Butiama mkoani Mara. Alisema hiyo ni mara ya tano wanasafiri kwa baiskeli kwenda mkoani humo. Tofauti na miaka mingine, alisema msafara wa mwaka huu unahusisha washiriki kutoka mataifa mengine matano mbali na Watanzania. "Katika msafara wa mwaka huu tutakuwa na wenzetu kutoka Rwanda, Burundi, Malawi, Jamhuri ya Demokrasi ya Congo na Kenya," alisema. Kadhalika, alisema safari ya mwaka huu itakuwa na mmoja wa washiriki wadogo zaidi Anuari Makumba (11) na wazee wawili wenye umri wa miaka 71 na 77. Katika msafara wa mwaka huu, alisema wanalenga kuenzi mchango wa Mwalimu Nyerere katika elimu, afya na mazingira. Kulingana na Landa, upandaji miti, kuchangia madawati katika shule mbalimbali na kuhamasisha upimaji afya ni miongoni mwa shughuli zitakazofanyika katika Mikoa ambayo msafara huo utapita. Safari hiyo iliyoanza leo, Oktoba 1, 2023 kwa mujibu wa Landa, inatarajiwa kukoma Oktoba 14, mwaka huu.
Benki ya Dunia inachunguza tuhuma za mauaji, ubakaji na kufukuzwa kwa nguvu kwa wananchi wanaoishi k
Benki ya Dunia inachunguza tuhuma za mauaji, ubakaji na kufukuzwa kwa nguvu kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya karibu na hifadhi zilizofadhiliwa na mradi wa utalii wa REGROW wa benki hiyo. Mzizi wa uchunguzi huo, ni tuhuma zilizoibuliwa dhidi ya benki hiyo, ikidaiwa kuwezesha matukio hayo katika Hifadhi ya Ruaha, kwa kuwa mfadhili wa mradi huo, unaogharimu Dola za Marekani 150 milioni (zaidi ya Sh375.7 bilioni). Mradi wa Regrow ulizinduliwa nchini mwaka 2018, ukitekelezwa kwa miaka sita hadi mwaka 2024, huku lengo lake ni kusimamia maeneo yaliyohifadhiwa na kukuza utalii wa asili katika Kanda ya Kusini mwa Tanzania. Kupitia mradi huo, hifadhi ya Ruaha iliyopo kilomita 130 kutoka Mji wa Iringa, inatarajiwa kuongezewa ukubwa karibu mara mbili ya ule wa sasa. Kulingana na watafiti wa Taasisi ya Oakland Thinkland, wanakijiji walieleza kuwa, askari wa wanyamapori waliwauwa wavuvi, kuwapiga wananchi, kuwabaka wanawake na kutaifisha maelfu ya ng’ombe kwa sababu wamevamia hifadhi ya taifa. Ripoti ya utafiti huo, iliyochapishwa alhamisi iliyopita inabainisha walinzi waliripotiwa kumpiga risasi mvuvi, William Nundu na kudaiwa kuwauwa wafugaji wawili, Sandu Masanja na Ngusa Salawa. “Kamanda wa polisi mkoani humo alidai watu hao waliuawa na wanyama pori wakati wakiingia ndani ya hifadhi kinyume cha sheria,” imeeleza sehemu ya ripoti hiyo. Ripoti hiyo, ilikwenda mbali zaidi na kueleza, zaidi ya watu 21,000 kutoka katika vijiji kadhaa vinavyozunguka hifadhi hiyo wanakabiliwa na kufukuzwa na Serikali. Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Anuradha Mittal alisema “Mradi wa Regrow haulindi tena wanyamapori au uhifadhi. Badala yake, benki (WB) inafadhili ukuaji wa uchumi kandamizi na wenye vurugu kwa kuzingatia kuongeza mapato ya utalii.” Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, WB ilipaswa kuchunguza rekodi ya Serikali ya Tanzania kuhusu haki za binadamu kabla ya kuifadhili. “Serikali iliidhinisha uondoaji wa watu karibu na eneo hilo hilo mwaka 2006 na imekosolewa kwa jinsi ilivyoshughulikia ufurushaji wa watu kwa lazima kaskazini mwa Tanzania uliotaka kuzua taharuki nchini humo kabla ya benki kuamua kufadhili mradi huo," aliongeza Mittal. Alisema "badala yake, ilionekana kwa njia nyingine na inaendelea kufanya hivyo. Inapaswa kuwajibishwa.” Ripoti ya taasisi hiyo inaendelea kueleza, wanakijiji waliambiwa kufikia Oktoba 2022 watalazimika kuacha ardhi yao licha ya kuwa na hati miliki, ambazo Serikali imezifuta kwa maelezo kuwa mali hiyo iko ndani ya mipaka ya hifadhi ya taifa. Hata hivyo, uamuzi huo ulipingwa na zaidi ya wanakijiji 850 wamepinga kufukuzwa katika mahakama kuu ya Tanzania, kama inavyoelezea ripoti hiyo. Mkazi mmoja wa Loliondo kwenye umbali wa kilomita 1,000 kutoka Ruaha, alieleza kupigwa risasi na maofisa usalama wa Tanzania, huku wapinzani wakisema vurugu hizo pekee zilitosha kuistua benki ya dunia iache kufadhili mradi huo. Wanakijiji wawili kwa usaidizi wa taasisi hiyo, wamewasilisha malalamiko yao kwa benki ya dunia wakisema hawakuarifiwa awali kwamba kufukuzwa kutakuwa sehemu ya mradi wa Regrow. Kiongozi wa moja ya jumuiya aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina, alisema jamii katika vijiji zaidi ya 40 hivyo inapoteza ardhi ya wazee wao, wanayoimiliki kihalali.
Mageuzi ya utendaji katika balozi, intelejensia ya masoko na mageuzi ya mfumo wa uchumi ni miongoni
Mageuzi ya utendaji katika balozi, intelejensia ya masoko na mageuzi ya mfumo wa uchumi ni miongoni mwa matarajio ya Tanzania, baada ya kuimarishwa kwa kitengo cha diplomasia ya uchumi cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Matarajio hayo, yanatokana na uamuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kukiimarisha kitengo hicho akimteuwa Balozi John Ulanga na Balozi Said Yakub kwenda kuifanya kazi hiyo. “Ndani ya Wizara hii (Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki) kuna kitengo cha diplomasia ya uchumi, lakini bado tukaona hakina nguvu, tukaona sasa tuanze kukijenga kitengo cha diplomasia ya uchumi. “Na kwa hiyo, tumeangalia CV mbalimbali tumeona CV yako Balozi Ulanga na Balozi Said kwamba zinaweza kwenda kuweka nguvu kwenye eneo hili, tumeona mnaweza kumtia joto sana Waziri (January Makamba),” alisema Rais Samia alipowaapisha viongozi mbalimbali aliowateuwa Septemba 26, mwaka huu. Kulingana na wataalamu wa diplomasia na wachumi, uamuzi huo ni turufu kwa Tanzania kwani kitengo hicho kitaweka msisitizo kwenye upatikanaji wa fursa kupitia diplomasia ya uchumi. Diplomasia ya uchumi ni nini Akizungumza na Mwananchi jana, Mtaalamu wa Diplomasia kutoka Chuo cha Diplomasia Tanzania, Innocent Shoo aliitafsiri diplomasia ya uchumi kuwa ni uhusiano baina ya nchi moja na nyingine katika masuala ya uchumi. Masuala hayo ya kiuchumi, kwa mujibu wa Shoo yanahusisha biashara na uwekezaji. “Tafsiri nyepesi ya diplomasia ya uchumi inanzia kwenye diplomasia ambayo maana yake ni uhusiano baina ya nchi moja na nyingine, au Shirika la taifa moja na lingine. “Ili hiyo diplomasia iwe ya kiuchumi, lazima kuwepo na uhusiano wa nchi moja na nyingine au Shirika la taifa moja na lingine katika masuala ya kiuchumi, yaani biashara au uwekezaji,” alisema. Mageuzi katika balozi Kuhusu kuimarishwa kwa kitengo cha diplomasia ya uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alisema kutaleta mageuzi ya utendaji wa balozi za Tanzania. Shoo ambaye pia ni Meneja wa Uhusiano kwa Umma wa chuo hicho, alifafanua mageuzi hayo ni kutoka kwenye utendaji wenye mrengo wa kisiasa na kugeukia uchumi. “Balozi nyingi hapo awali zilikuwa zikifanya shughuli zake kwa sura ya kisiasa, lakini kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na haja ya mageuzi kutoka utendaji huo na kufanya kazi kwa kusaka fursa za kiuchumi,” alisema. Aliufafanua utendaji huo wa kiuchumi, unahusisha kuzisaka fursa zilizoko katika mataifa mengine kwa ajili ya Tanzania, zikiwemo za kibiashara, uwekezaji na kiuchumi kwa ujumla na kwamba hiyo ndiyo kazi ya kitengo hicho. “Kama unakumbuka Rais Samia Suluhu Hassan, amekuwa akiwaambia mabalozi wafanye mbinu za kuleta wawekezaji, anawaambia wawaambie kwamba Tanzania ina nini na nini,” alisema. Kwanini muhimu Kuimarishwa sasa kwa kitengo hicho, Shoo alieleza kunatokana na ukweli kwamba zipo fursa lukuki zimeingia katika diplomasia ya uchumi, ikiwemo uchumi wa kidigitali, uchumi wa buluu, uhifadhi wa mazingira na utalii. “Diaspora ni fursa nyingine, kwa hiyo kitengo hicho kitakwenda kutafsiri hayo na kuhakikisha diaspora wanashirikishwa ili wawe na tija kwa nchi,” alisema. Kwa mujibu wa Shoo, kitengo hicho ni turufu kwa Tanzania katika intelejensia ya masoko, yaani nchi itakuwa na uwezo wa kujua bidhaa gani inatakiwa kuuzwa wapi na kwa kiasi gani,” alisema. “Hii itawawezesha hata wakulima wetu, wajue wanalima nini na kiasi gani kwa ajili ya soko la wapi, kwa kuwa intelejensia ya masoko itatusaidia,” alisema. Kitatatua changamoto Akizungumzia hilo, Mhadhiri wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa Aurelia Kamuzora alisema pamoja na Tanzania kuwa na sera inayotaja masuala ya diplomasia ya uchumi, lakini kulikuwepo changamoto za utekelezaji wake. Alizitaja changamoto hizo mageuzi kutoka mfumo wa uendeshaji uchumi kijamaa hadi uchumi unaotegemea mitaji yaani uchumi wa kibepari, ambao ndiyo utaratibu wa duniani kote. “Kwa hiyo kitengo hicho kitatusaidia kujipanga kueleza namna gani nchi yetu inaweza kuuendea uchumi wa kutegemea mitaji badala ya ujamaa kwa maana kutegemea Serikali pekee ndiyo iwekeze,” alisema. Lakini, alisema mageuzi hayo yanayoendelea kufanyika, bila shaka yataambatana na sera zitakazotumika na wanaoitangaza Tanzania kuieleza dunia kuwa kwa sasa imebadilika. “Kuna wakati tunakwama kwa sababu nchi nyingine zinaamini sisi ni wajamaa, kwa mfano sasa nipo India tunawaeleza kwamba Tanzania inaweza kulima kilimo cha kahawa kwa mikataba. “Wanatuhoji inawezekanaje wakati mazao yote ya Tanzania yanamilikiwa na Serikali na kama tunalima kwa mikataba kwa sera ipi, haya ndiyo mambo ambayo kitengo hicho kitatusaidia kuyaweka sawa,” alieleza. Kulingana na mhadhiri huyo, kitengo hicho kitaisaidia Tanzania kutengeneza lugha moja itakayotumika na mabalozi na wawakilishi wengine wa Tanzania nje kuhusu kuitangaza nchi. “Unahitaji utengeneze diplomasia ya uchumi ili ipange sera itakayotumika kwa mataifa yote, waelewe kitu kinachoendelea kuwepo kwa lugha moja,” alisema. Dalili njema Mhadhiri wa Mahusiano ya Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Muhidin Shangwe alieleza kuimarishwa kwa kitengo hicho ni dalili ya kuwepo mwamko zaidi wa utekelezaji wa diplomasia ya uchumi nchini. Kulingana na Shangwe, diplomasia ya uchumi ilikuwepo tangu miaka mingi iliyopita na iliwekewa msisitizo zaidi katika Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001. “Kuimarishwa kwa kitengo hicho kunaweka msisitizo wa kuifanya Tanzania inufaike zaidi kiuchumi kupitia mahusiano yake na mataifa au mashirika ya kimataifa,” alisema. Akihojiwa katika moja ya kituo cha runinga nchini, Balozi John Ulanga alisema kipaumbele ni kutekeleza mkakati wa diplomasia ya uchumi ndiyo kazi atakayoanza nayo. “Tumeelekezwa kuhakikisha mkakati wa utekelezaji wa diplomasia ya uchumi unakamilika na kujulikana ndani ya Serikali na sekta binafsi,” alisema.
Wakazi wa Kijiji cha Mwabasabi, wilayani Buchosa Mkoa wa Mwanza, wameeleza namna Mpango wa Kusaidia
Wakazi wa Kijiji cha Mwabasabi, wilayani Buchosa Mkoa wa Mwanza, wameeleza namna Mpango wa Kusaidia Kaya Masikini (TASAF) ulivyogeuza maisha yao kutoka hali duni hadi nzuri. Akizungumza kijijini hapo, Ernest Ezary alisema kabla ya TASAF alikuwa na maisha magumu kiasi cha kushindwa kulipa kodi ya nyumba aliyokuwa akiishi. Alisema ilikuwa vigumu kwake na familia yake kupata huduma muhimu kutokana na hali ngumu ya maisha iliyokuwa ikimkabili. “Nilifukuzwa kwa kushindwa kulipa kodi ya nyumba, TASAF ilivyokuja nilikidhi vigezo nikasajiliwa, nikaanza kupata malipo, yamenifanya nitoke katika hali ngumu na kuelekea katika unafuu,” alisema. Alisema kwa sasa angalau amehifadhi fedha zilizomwezesha kulima shamba na kupata mazao kwa ajili ya chakula na biashara. Hatua hiyo, alieleza imamwezesha kufanya biashara ya mazao ambapo kwa sasa ananunua mpunga kutoka kwa wakulima wengine na kuuza. Kulingana na Ezary, kwa sasa amefanikiwa kujenga nyumba na hivyo maisha yake yamebadilika kutoka kufukuzwa kwa kukosa kodi ya nyumba hadi kumiliki nyumba yake. “Naishukuru TASAF lakini nimshukuru pia Rais Samia Suluhu Hassan, Naomba atutazame na aongeze nguvu na bidii tujikwamue zaidi,” alisema. Mkazi mwingine wa kijiji hicho ni Elizabeth Seleli aliyesema TASAF imemwezesha kukodi majaruba na hatimaye akawa na eneo lake analolitumia kwa kilimo cha mpunga. Alieleza kilimo hicho kilichotokana na fedha alizopata TASAF zimemwezesha kujenga nyumba na sasa anamiliki mji wake. Mweka Hazina wa Kikundi cha Wapendanao kijiji hapo, Damari Manyirezu alisema kabla ya TASAF walikuwa na amana ya Sh10,000 lakini baada ya kuwekeza kwa fedha za mpango huo kwa sasa kikundi kina amana ya Sh800,000 Alisema hatua hiyo imetokana na uwekezaji wa fedha kutoka kwa wanachama, ambao wote ni wanufaika wa TASAF. “Kwa sasa tunakopeshana kwenye kikundi hiki na imetuwezesha kujenga baadhi, kwa mfano mimi nimejenga,” alisema. Sikujali Baraka ni mnufaika wa kikundi hicho, alisema kwa sasa ameanza kujenga kutokana na mikopo mbalimbali anayochukua kwenye kikundi hicho. Alieleza kabla ya hapo, alikuwa na maisha magumu kiasi kwamba asingeweza kumudu hata fedha ya pango la nyumba, lakini TASAF imemkomboa.
Hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko ya ghafla na mara kwa mara ya viongozi, imetajw
Hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko ya ghafla na mara kwa mara ya viongozi, imetajwa kuakisi mvurugano ndani ya Serikali yake, huku ikiwajaza hofu ya kudumu kwenye mamlaka watendaji wake. Kulingana na viongozi waandamizi wa Utumishi na wanazuoni, mvurugano huo unasababishwa na kasoro katika mamlaka ya uteuzi, inasisitiza umuhimu wa Katiba Mpya na kuonyesha dosari katika kufanya teuzi kwa kuzingatia itikadi za kisiasa. Msingi wa hoja ya mvurugano, unajengwa na hatua za hivi karibuni za Rais Samia, kuteuwa na kutengua viongozi ghafla, kadhalika kuwahamisha wengine hata kabla hawajajipanga kutekeleza majukumu yao. Hata hivyo, mkuu huyo wa nchi ameweka wazi baadhi ya sababu za uamuzi huo, akitaja kukosa taarifa za watendani ndiko kunakofanya awaondoe baadhi yao. Akihutubia baada ya hafla ya kuwapisha wateule wapya jana, Rais Samia alisema, “Tunaomba mtuletee taarifa za mnayoyafanya humo ndani, saa nyingie unaweza ukaamua lakini hujui unayemuondoa amefanya kazi gani. “Lakini tukiwa na taarifa zenu hapa unapopanga na kupangua unaweza kusema hapana huyu asitoke anaendelea kufanya kazi vizuri, kwa hiyo kijana niliyemuondoa TTCL kumbe alishafanya kazi nzuri sana baadaye sasa ndiyo Mwneyekiti wake wa bodi ananiletea taarifa,” alisema. Maana halisi ya mvurugano inatokana na kilichofanywa Septemba 24, mwaka huu, Rais Samia alipomteuwa Maharage Chande kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), siku moja baadaye alitengua uteuzi wake na kumteuwa kuwa Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania. Hii si mara ya kwanza, Rais Samia kufanya mabadiliko hayo ya ghafla, alifanya hivyo Agosti 30, mwaka huu, alipomteuwa Profesa Kennedy Gaston kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Septemba 1, mwaka huu aliapishwa katika wadhifa huo. Lakini siku tatu baadaye, Septemba 3, mwaka huu uteuzi wake ulitenguliwa na aliteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Jambo kama hilo, lilitokea pia kwa Alexander Mnyeti aliyeteuliwa Septemba 30, mwaka huu, kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, lakini kabla ya kuapishwa alihamishiwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Hata Thobias Mwesiga alikumbana na hilo, Aprili 4, 2021, alipoteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kabla ya kuapishwa kesho yake alitenguliwa na James Mataragio aliteuliwa kuendelea na nafasi hiyo. Dk Raphael Chegeni naye, aliuonja wadhifa wa Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa siku tatu, kuanzia Julai 28, mwaka jana hadi Julai 31, mwaka huo alipotenguliwa na nafasi yake kuchukuliwa na Meja Jenerali Suleiman Mzee. Kama hiyo haitoshi, katikati ya uapisho, David Kafulila alihamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, badala ya Arusha na John Mongela akipelekwa mkoani humo, ikiwa ni siku mbili baada ya kuteuliwa. Pamoja na mifano hiyo, wapo mawaziri lukuki waliohamishwa kutoka wizara moja kwenda nyingine, akiwemo Mohammed Mchengerwa kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenda Ofisi ya Rais, Tawala za Rais na Serikali za Mitaa (Tamisemi) akibadilishana na Angella Kairuki. Uhamisho pia, ulimkumba Dk Damas Ndumbaro aliyetoka Wizara ya Katiba na Sheria na sasa ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Dosari kwa mamlaka ya uteuzi Akizungumza na Mwananchi kuhusu uamuzi hayo, Katibu Mkuu wa zamani wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ruth Mollel alisema hali hiyo inaonyesha uwepo wa dosari kwa mamlaka ya uteuzi. Dosari hiyo inatokana na kile alichoeleza, inashindikana kufanyika uchunguzi wa kutosha kwa anayetarajia kuteuliwa, hivyo mamlaka ya uteuzi inajikuta imeamua ikiwa na taarifa chache. Lakini hilo, linathibitishwa na kauli ya Rais Samia alipowaapisha viongozi hao alisema, “Maharage Chande niliona TTCL panakufaa zaidi, sasa baadaye nikagundua una biashara ndani ya TTCL, nikaona sasa nikupe Postamasta Mkuu.” Kwa upande mwingine, Ruth alieleza kiongozi itamchukua mwaka mmoja au mmoja na miezi mitano kuielewa vema taasisi na kutengeneza njia ya utendaji, hivyo akitenguliwa mapema ni vigumu kuona matokeo ya kazi yake. Mabadiliko hayo ya mara kwa mara, alisema yanaathiri utumishi wa umma, huku akieleza angalau kwa mawaziri sio tatizo kwa kuwa sehemu kubwa ya kazi zinaendeshwa na watendaji. Kulingana na Ruth, mabadiliko hayo ni kikwazo cha kujiamini kwa watendaji hao, muda mwingi wanahofu iwapo wataendelea kutumikia nafasi walizonazo. “Hii inafanya watu wasitulie, unatakiwa mtu ukae kwenye nafasi ukiwa vizuri, lakini unakaa kama umekaa upande hujui utaondolewa saa ngapi, hii sio sawa,” alisema. Suluhu ya yote hayo, alisema kuzingatia nafasi za utendaji wasipewe watu kwa kigezo cha itikadi za kisiasa, wapewe wenye uwezo na eneo husika. Lakini, alipendekeza kuandaliwa mapema kwa viongozi wanaotarajiwa kuteuliwa kupitia mafunzo maalum, kisha wakati wa uteuzi mamlaka izingatie kanzidata ya waliofunzwa. “Rais apelekewe majina matatu afanye uchaguzi wa nani anaona anafaa kuwa kwenye nafasi husika, hiyo itakomesha leo umempeleka huyu kesho yule,” alisema. Kuna changamoto ya kukosekana umakini kwa mamlaka ya uteuzi, kama anavyoeleza Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Mohammed Bakary. Alieleza uchunguzi wa anayeteuliwa unapaswa kufanyika kwa kina kujua taarifa zake kulingana na eneo analotarajia kwenda kulisimamia na asipewe nafasi kwa taarifa nusu nusu. “Unapoteuliwa kuna ufuatiliaji mkubwa unaotakiwa kufanywa ili kuhakikisha unateuwa watu wanaoendana na kazi unayoitarajia,” alisema. Usiri ni tatizo Kasoro nyingine kwa mamlaka ya uteuzi, alisema inatokana na pale inapoamua kumteuwa mtu kwa siri, bila kumdokeza ndiyo sababu wanatokea wanaogomea teuzi baada ya kuteuliwa. “Utaratibu wa kawaida mtu anayeteuliwa anakuwa na taarifa za kitakachoendelea lakini kukiwa na usiri kunakuwa na changamoto na wakati mwingine hata mtu anaweza kukataa,” alisema. Kuhusu mabadiliko ya mara kwa mara, alieleza yanawavunja moyo watendaji kwani pamoja na mipango mizuri wanayopanga huwa wanakosa imani iwapo watafanikiwa kuitekeleza wakiwa katika ofisi hiyo. “Kidogo inaweza kuleta hali ya kupoteza kujiamini, hata taasisi au wizara husika inakwama kwa sababu akija huyu kabla hajatekeleza lengo anaondoka anakuja mwingine wakati anajipanga anaondolewa,” alisema. Ingawa kwa hayo yote, alisema mamlaka ya uteuzi haipaswi kulaumiwa, kwa kuwa mara nyingi wanaotenguliwa huonekana hawajafanya vizuri au zimepatikana taarifa mbaya kumuhusu. “Inawezekana taarifa mbaya kumhusu mtu husika zimepatikana baada ya kuteuliwa, hiyo inaishawishi mamlaka ya uteuzi kufanya mabadiliko,” alisema. Mvurugano Hoja hiyo imemuibua, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyesema kinachoendelea kinathibitisha kuwa CCM na Serikali yake haijui inapoipeleka nchi. “Tunaona ni bandika bandua na suluhisho la hili ni kuwa na Katiba mpya ili kuwa na mifumo madhubuti ya uteuzi,” alisema. Kwa hali ya sasa ya uhaba wa dola, mgawo wa umeme na gharama za maisha, Mbowe alitarajia Serikali ijielekeze kwenye kutatua hayo, lakini imejikita kuteunga na kutengua akisema, “ni mvurugano tu.” “Tunasisitiza tubadili Katiba ili kubadili mifumo ya nchi, tunaona CCM imepoteza uelekeo, wanachukuliwa makada wa CCM wanapelekwa katika utumishi wa umma. Kuna utaratibu wa kuwaingiza watu katika utumishi wa umma na kuwapandisha madaraja, sasa wanapelekwa kuwa wakurugenzi wa halmashauri, katika mambo kama hayo fedha zikiibiwa na kuvurugwa utamlaumu nani,” alisema Mbowe. Alisisitiza hoja ya Ruth kuwa, uteuzi unafanyika kisiasa akisema, “uteuzi wa nafasi za watumishi wa umma, umekuwa wa kisiasa, haueleweki, kila siku mtu anateuliwa, tunahamisha watu kwa kuwateua mabalozi, sasa tutateua mabalozi wangapi.” Alisema katika kipindi cha takribani miaka miwili ya Rais Samia, “ameunda wizara mpya, unaongeza gharama za uendeshaji, sasa unajiuliza tatizo lipo kwa washauri wake au kina nani? Kwa kifupi Serikali imevurugwa, CCM imevurugwa na msaada unaoweza kuwasaidia ni kupata Katiba mpya.” Kwa kinachoendelea sasa, alisema watumishi hawajiamini kwa kuwa hawajui watafukuzwa, kuhamishwa, kusimamishwa au kuteuliwa lini.
Umewahi kujiuliza kwanini baadhi ya bunifu na tafiti nchini zinaishia kabatini? Kama haukuwahi kuji
Umewahi kujiuliza kwanini baadhi ya bunifu na tafiti nchini zinaishia kabatini? Kama haukuwahi kujiuliza bila shaka umewahi kusikia kilio cha wabunifu kuhusu kukosekana utashi wa kuendelezwa kwa bunifu zao. Kumbe, swala si bunifu na tafiti kuwekwa kabatini, kilichomo ndani yake ndicho kinachoamua matokeo yake kama anavyoeleza Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia nchini (Costech), Dk Amos Nungu. Katika mahojiano maalum na Gazeti hili, Dk Nungu anaeleza uwepo wa wabunifu wanaoshindwa kufikiri mahitaji ya soko na mazingira ya eneo walilopo. Kwa sababu hiyo, anasema wanajikuta wakifanya bunifu zisizo na tija kulingana na mazingira ya eneo husika na hivyo, kushindwa kuendelezwa. Sio kwamba wanachokiwaza si kizuri, Dk Nungu anasema changamoto ni kuendana na mazingira ya Tanzania ili apatikane mlaji. "Ubunifu ni namna ya kufanya kazi ili ulete tija, unapobuni hakikisha kuna mlaji, kama hakuna mlaji utapeleka wapi huo ubunifu. "Inatakiwa kuja na kitu ili wananchi wakitumie, mwingine anabuni kitu kinachomlazimu mtumiaji aingie gharama kubwa, kwa hiyo bunifu hizi mara nyingi zinakosa soko," anaeleza. Bunifu nyingine zinazoishia kabatini, anasema ni zile ambazo ili kuendelezwa zinaihitaji Serikali ifanye uwekezaji mkubwa, akitolea mfano ububifu wa kijana aliyewahi kuunda helikopta. "Sawa amebuni helikopta, itatumikaje na tutazitumia wapi, ili itumike inahitaji vibali vingi vya Kimataifa na ili iruhusiwe kuruka kunahitajika mambo mengi na uwekezaji mkubwa. "Vinginevyo utabaki ubunifu wa kuonyesha wengine kuwa inawezekana lakini hautumiki na hawezi kupata soko," anasema. Mkurugenzi huyo anasisitiza umuhimu wa bunifu kuzingatia mahitaji ya jamii na ziwe zile zitakazoleta suluhisho na kuwepo uwezekano wa kutumika. Anatolea mfano baadhi ya bunifu ikiwepo ile ya kutengeneza tofali za plastiki, akisema bei yake ilikuwa kubwa zaidi ya tofali zilizopo, jambo linalosababisha kukosa soko. Hata hivyo, anasema hakuna malighafi ya kutosha kuzalisha tofali nyingi ili kuendana na mahitaji ya soko. "Sawa ubunifu umesaidia kupunguza taka za plastiki, lakini hautumiki kwa sababu hauna mlaji, kuna mbadala wa tofali za bei rahisi, huyu aliyebuni atapeleka wapi tofali zake," anasema. Kwa mujibu wa Dk Nungu, yupo mbunifu aliyebuni gari kutoka Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), akisisitiza ni ubunifu unaoishia kujenga hamasa lakini si kutumika nchini. "Kweli ubunifu wake umetumika kuhamasisha wengine, lakini hawezi kupata soko kwa hiyo anaishia kuwa mbunifu lakini hapati tija ya alichokifanya," anasema. Costech lawamani Aina hiyo ya bunifu, Dk Nungu anasema ndizo zinazoiingiza Costech na Serikali kwa ujumla kwenye wimbi la lawama kwamba hazina utashi wa kuendeleza. Wabunifu wengi, anasema wamekosa uelewa wa kuzingatia mahitaji ya wakati na mazingira na hivyo kujikuta wanailaumu Serikali. "Tunalaumiwa mbona hamuendelezi, kuendeleza Serikali haifanyi biashara, ukitaka kumuendeleza kwa kuhamasisha sawa lakini kufanya biashara inahitaji mtaji. "Mtu hawezi kufikiria kununua gari hii ya mbunifu kutoka hapa, akaacha kutoka maeneo ambayo tayari kuna viwanda ambavyo mtu angeweza kupata gari kwa bei nafuu," anasema. Anaeleza tatizo la baadhi ya wabunifu hawaangalii kwa jicho pana wanataka kubuni vitu ilimradi waonekane wamebuni, lakini si kutafuta soko lake. Hali iliyopo kwenye bunifu, haitofautiani na katika tafiti, Dk Nungu anasema nyingi zinafanyika ili kutimiza malengo fulani ndiyo maana zinaishia makabatini. Mathalan, baadhi ya tafiti anasema zinafanyika kwa sababu ni takwa muhimu kwa kila mwanafunzi ili ahitimu masomo yake ya elimu ya juu. Kwa sababu hiyo, anasema zinafanyika tafiti zinazolenga kufanikisha kuhitimu masomo lakini si kutumika kupata ufumbuzi wa masuala mbalimbali kwenye jamii. "Kwa sababu ilikuwa lazima afanye utafiti ili amalize elimu kwa hiyo wakati mwingine anakaa na mkufunzi wake wanaunda utafiti ambao utaonyesha huyu mwanafunzi kweli kaiva kulingana na mtalaa na mara nyingi huwa si halisia, ndiyo maana zinaishia kwenye makabati," anasema Zipo tafiti anazisema zimewahi kuwa na tija katika taifa, ukiwemo ule wa kubaini usalama wa dawa ya kikombe cha babu kilichokuwa kinatokewa Loliondo mkoani Arusha. Anaeleza kulikuwepo na hofu ya usalama kwa binadamu kwa dawa hiyo, hivyo Costech ililazimika kutoa fedha kwa Mamlaka ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR). Anaeleza utafiti huoz ulibaini kuwa dawa hiyo ni salama kwa matumizi ya binadamu na iliendelea kutumika. "Hata mwaka juzi Serikali iliposema Chikichi ni zao la kimkakati tulitoa fedha kuipatia, Taasisi ya utafiti wa Kilimo (TARI) ikatafiti mbegu bora za zinazokomaa kwa muda mfupi, ni utafiti unaotumika hadi sasa," anasema. Lakini, anasema hayo yote yanasababishwa kukosekana kwa fedha za kufanyia utafiti hasa zile za wanafunzi. "Ili afanye utafiti wenye soko atahitaji fedha ya kwenda eneo la tukio na kufanya utafiti," anasema. Anaeleza utaratibu wa sasa wa tume hiyo ni kumjua mlaji wa tafiti kabla ya kutoa ufadhili wa fedha. Changamoto Pamoja na mawazo mazuri wanayowasilisha vijana kwa tume hiyo, anasema yapo yanayohitaji kuboresha, lakini mara nyingi hawakubali. "Vijana wanakuja na mawazo yao ni mazuri sana, kuna wakati unawashauri kwamba hili halina uendelevu, lakini kijana hakuelewi. "Unamwambia hili wazo Marekani lingekuwa zuri kulingana na mazingira yao, kijana anakwambia hujui tu unanibania," anasema. Vijana kuunda vikundi vya ubunifu anaitaja kuwa moja ya mbinu za kuzalisha bunifu zitakazokuwa na tija kwa jamii. Hata wawekezaji, anasema wangependa kukutana na kikundi cha watu, kwa kuwa wengi hawaamini uendelevu katika mtu mmoja. "Wakiwa wengi huyu ana ujuzi huu na yule ana mwingine, watasaidiana katika mawazo, lakini akiwa mmoja hawezi kuwa na utaalamu wa masoko. Tatizo vijana wengi hawataki kujiunga katika vikundi anaona ubunifu wake utamtaifisha mwingine," anasema. Kinachofanywa na tume hiyo, Dk Nungu anasema ni kuwapokea vijana na kuwashauri kuhusu bunifu zao, wapo wanaoandikiwa barua za utambulisho kwa taasisi zinazohusika na walichokibuni. Pamoja na kufanyiwa hivyo, wapo wasiokuwa tayari kukubaliana na ukweli kwamba bunifu zao hazitumiki, wanang'ng'ana na kujikuta wanakosa uendelevu. Katika maelezo yake, Dk Nungu anasema kumekuwepo na changamoto nyingine za kwamba Costech inazima ndiyo za wabunifu. Anatolea mfano mbunifu aliyewahi kuunda Kituo cha redio, anasema alizuiwa na Serikali. "Anaporusha mitambo yake akapata muingiliano na mtu ambaye kalipia leseni yake hapo itakuwa kero na inabidi azuiwe," anasema. Anasema kwa sasa wameingia makubaliano na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), akitokea mbunifu wa masuala yanayodhibitiwa na mamlaka hiyo na Costech ikijiridhisha na tija ya ubunifu husika, ataombewa kibali cha majaribio kwa miezi mitatu. "Kama hajaridhika anapewa nyongeza ya muda wa miezi mitatu mingine, Serikali inajaribu kuwafikia ili tusiwakatishe tamaa," anasema. Mitalaa mipya tumaini Dk Nungu anasema maboresho ya mitalaa ni tumaini jipya la mafanikio ya Tanzania katika eneo la ubinifu. Kwa sababu, anasema mitalaa hiyo inamjenga kijana tangu mdogo katika kipaji chake, hivyo kutakuwa na uendelevu. "Kutokana na hii mitalaa mipya huyu kijana aliyetengenza nyumba ya ghorofa ya maboksi atapelekwa kwenye elimu ya ufundi," anasema.
Makali ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mc
Makali ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa yameanza na watumishi saba wa Halmashauri ya Liwale mkoani Lindi, baada ya kuagiza wachukuliwe hatua za kinidhamu. Agizo la hatua dhidi ya watumishi hao, lilitolewa jana kupitia barua ya Mchengerwa iliyosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikali Ntenghenjwa Hosseah, ikimtaka Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Sospeter Mtwale awachukulie hatua. Huu ni mwanzo wa makali ya mwanasiasa huyo, tangu alipoapishwa kuwa Waziri wa Tamisemi Septemba 1, mwaka huu nafasi ambayo Rais Samia Suluhu Hassan alimsifu kuwa anaimudu. Kabla ya hatua hiyo, juzi akiwa katika ziara ya Rais Samia wilayani Nachingwea, Mchengerwa alisema ataendelea kuhakikisha watumishi katika halmashauri wanasimamia vema miradi ya maendeleo na kuwachukulia hatua watakaokwamisha. Katika maelezo yake hayo, alitolea mfano hatua za kinidhamu anazotarajia kuzichukua kwa watumishi saba wa halmashauri ya Liwale, ambao leo ndiyo amewatangaza rasmi. Kulingana na barua hiyo iliyotolewa jana, watumishi watakaochukuliwa hatua hizo ni Sisty Nyau (Kaimu Mhandisi wa Wilaya), Damas Mumwi (Mkuu wa Idara ya Kilimo na Ushirika) na Vinsent Moyo (Mkuu wa Idara ya Ugavi na Manunuzi). Wengine ni Mohamedi Songolo (Mkuu wa Idara ya Tehama), Sadick Khatibu (Katibu wa Afya) na Tunu Mtamaha (Ofisa Ugavi na Ununuzi aliyehamishiwa halmashauri ya Wilaya ya Kilwa). Sababu ya hatua hizo, kulingana na barua hiyo ni kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo hivyo, kuzorotesha utendaji kazi wa shughuli mbalimbali za halmashauri hiyo. “Waziri Mchengerwa ameelekeza hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa mujibu wa Kanuni ya 42 ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022 inayoainisha kuwashusha vyeo. “Kukatwa mshahara kwa asilimia 15 kwa muda usiopungua miaka 3 pamoja na kufukuzwa kazi iwapo watabainika kufanya makosa hayo,” ilieleza sehemu ya barua hiyo. Mbali na hatua dhidi ya watumishi hao, Mchengerwa alielekeza kusimamishwa kazi, badala ya kuhamishwa kwa maofisa wote wenye kesi za rushwa na ubadhirifu hadi mashauri yao yatakapokamilika. “Ofisa yeyote mwenye kesi ya uhujumu uchumi au ubadhirifu wakati kesi yake ikiendelea ataendelea kuchunguza mienendo yake na hukumu yake ikitoka hatopewa tena jukumu la Ukuu wa Idara au Kitengo,” alisema.
Kitendawili cha mpango wa afya kwa wote nchini, kinatarajiwa kupata majibu Oktoba mwaka huu, katika
Kitendawili cha mpango wa afya kwa wote nchini, kinatarajiwa kupata majibu Oktoba mwaka huu, katika hafla ya maadhimisho ya miaka 10 ya kongamano la Afya Tanzania (THS) litakalowakutanisha wadau wa sekta ya afya kutoka ndani na nje ya nchi. Kongamano hilo, litakalowakutanisha wadau 1,000 wa sekta hiyo, linatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia Oktoba 3 hadi 5, mwaka huu. Mjadala kuhusu mpango wa afya kwa wote, unakuja kipindi ambacho Shirika la Afya Duniani (WHO) limeripoti takriban nusu ya watu duniani hawawezi kuzifikia huduma za afya. Hayo ni matokeo ya kutokamilika kwa mpango wa afya kwa wote (UHC) ambao nchi wanachama wa WHO ikiwemo Tanzania zimekubaliana kuutekeleza kufikia 2030. Wakati mpango wa huduma za afya kwa wote ukiwa kitendawili Tanzania Bara, hali ni tofauti visiwani Zanzibar ambapo kila mwananchi anapata huduma za afya bure. Hayo yaliibuliwa jijini Dar es Salaam jana na Rais wa THS, Dk Omary Chillo katika warsha na waandishi wa habari kuelekea kongamano hilo. Alisema kongamano hilo, linabebwa na kauli mbiu ya ‘kuimarisha Mifumo ya Afya kwa ajili ya Huduma za afya kwa wote (UHC), ikilenga Huduma ya Afya ya Msingi (PHC). Alisema majadiliano yatakayofanyika yanapaswa kuihimiza jamii itafute taarifa kuhusu maendeleo ya mfumo wa afya na utekelezaji wa afua zinazolenga kufikia huduma kwa wote. "Tukio hili ni taswira ya kile kitakachojadiliwa wakati wa kongamano la afya ifikapo mwezi Oktoba. Kwa upande mwingine, majadiliano haya yanapaswa kuhimiza jamii kutafuta taarifa kuhusu maendeleo ya mfumo wao wa afya na utekelezaji wa afua zinazolenga kufikia Huduma ya Afya kwa Wote na Afya ya Msingi," alisema. Aliyataja mengine yatakayojadiliwa ni upatikanaji wa huduma ya afya ya msingi na uhitaji wa kuimarishwa kwa huduma za afya. Katika kuifikia huduma ya afya kwa wote, Dk Danstun Mshana kutoka Idara ya Afya, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) alisema Serikali ipo katika hatua mbalimbali za kuhakikisha inatekeleza mpango wa afya kwa wote. Miongoni mwa hatua za utekelezaji wa hilo, alisema Serikali imejenga vituo vya afya, Zahanati na Hospitali za Wilaya nchini. "Serikali katika kipindi cha miaka mitano pekee imejenga vituo vya afya zaidi ya 1,800, kumekuwa na nguvu kubwa katika ujenzi wa vituo vya afya, hospitali za Wilaya na Zahanati," alisema. Wakati Tanzania bara kukiwa na hali hiyo, visiwani Zanzibar hali ni tofauti kama inavyoelezwa na Mkuu wa Divisheni ya Utafiti, Wizara ya Afya Zanzibar, Rashid Maulid Rashid. Rashid alisema visiwani humo kupitia mfuko wa afya kwa wote, kila mwananchi anapata huduma za afya bure. "Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka huu mfuko wa afya, kila asiye na kipato anapata huduma bure za afya,” alisema. Alieleza katika mfuko huo, watumishi wa umma wanachangia asilimia 3.5 ya mishahara yao inayokatwa moja kwa moja, lakini wananchi wenye vipato vya chini hawatozwi chochote. Pamoja na hilo, alisema Serikali visiwani humo imefanikisha ujenzi wa miundombinu ya huduma za afya, hivyo kila katika kila kilomita tano kina Kituo cha afya. “Hii tumeifanya ili kulinda afya za wananchi. Lakini kwa sasa tuna hospitali za Wilaya karibu katika kila Wilaya tofauti na zamani zilikuwa mbili tu Unguja na Pemba,” alisema. Mkuu wa Mipango wa Shirika la Kimataifa la Girl Effect, Ritha Mbeba alisema katika kongamano hilo watajikita kuonyesha namna elimu ya afya ya uzazi kwa mabinti ilivyo na tija katika maisha yao.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa siku chache baada ya kuteuliwa kushika w
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa siku chache baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo, ameelekeza watendaji wake kutumia siku 100 kutatua migogoro yote ya ardhi nchini. Siku 100 ni sawa na miezi mitatu na siku 10 za uongozi wake ndani ya Wizara hiyo inayotajwa kuwa mfupa mgumu kwa mawaziri wengi waliowahi kuhudumu. Na hasa migogoro ya ardhi ndilo jambo linaloipa ugumu wizara hiyo, ndiyo maana napata wasiwasi juu ya utekelezwaji wa maelekezo haya. Sio kwamba namkatisha tamaa Waziri Silaa, lakini tukirejea uhalisia wa mwenendo wa migogoro ya ardhi nchini, napata wakati mgumu kuamini uwepo wa uwezekano wa kutatuliwa kwa siku 100. Migogoro hii hii iliyowashinda watangulizi wake lukuki na sio kwamba hawakuwa na mbinu za kuitatua bali ziligonga mwamba kutokana na uhalisia wa ugumu wake, mmh…! kwa siku 100 sina uhakika. Ngoja nikwambie kitu kaka… migogoro ya ardhi sio ile ya wakulima na wafugaji pekee, sio wanakijiji na hifadhi za taifa, sio mkulima na mkulima. Ugumu wa migogoro hii unakuja pale ambapo ardhi inayogombewa inamilikiwa mara mbili, mmoja wa wamiliki ni kigogo anayefanana nawe wadhifa na mwingine ni wananchi mathalan kijiji fulani. Tena katika aina hii ya migogoro, kijiji huwa na nyaraka zote halali za umiliki, lakini huyo anayefanana nawe wadhifa pengine ametumia mabilioni kumiliki. Kutatua aina hii ya migogoro inakubidi ama uamue kukosana na mtu mnayeketi vikao pamoja, kugonga mvinyo na mambo mengine au ukosane na wananchi ambao wakilia kwa mwajiri wako wadhifa wako unakomea hapo. Huu ni mfano mdogo wa mazingira yanayowabakiza njiapanda watendaji ndani ya wizara hiyo. Kama hiyo haitoshi, ipo migogoro unayotamani msaada wa watendaji ndani ya wizara ili ikatatuliwe na kwa bahati mbaya unayemtuma ana maslahi ndani yake. Badala ya kutatua anatengeneza mazingira ya kuvutia upande wake na hatimaye anachochea zaidi migogoro. Inakuhitaji kuwa kiumbe mwenye maamuzi magumu ili kufanikiwa kuikomesha migogoro hiyo ndani ya siku 100, lakini uwe tayari kukosana na baadhi ya watu ambao aghalabu mnakaa meza moja ya mazungumzo. Kwa mtazamo wangu, ukizitumia siku 100 kuweka mkakati wa kuhakikisha ardhi yote ya Tanzania imepimwa na ukafanikiwa, itachukua siku chache kumaliza migogoro ya ardhi. Migogoro mingi inachipuka kutokana na ardhi kutopimwa, hivyo kutoa mwanya kwa wajanja kuvamia au kutoa maburungutu kumiliki. Hili hufanywa pia hata na wananchi, kuna wakati wanavamia ardhi wanaiendeleza baadaye mwenyewe anapoibuka migogoro unaanza. Nimewahi kushuhudia migogoro kati ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania na mmiliki wa Vituo vya Mafuta vya Victoria, ambao kila mmoja alikuwa na vielelezo vinavyohalalisha umiliki wa ardhi hiyo katika moja ya maeneo jijini Dar es Salaam. Ulikuwa migogoro kati ya taasisi ya kidini inayojiweza kiuchumi, dhidi ya mtu binafsi anayejiweza pia, aliyebaki katikati alikuwa Waziri wa ardhi wa wakati huo (William Lukuvi). Hadi migogoro kulikuwa na mlolongo wa miezi kadhaa ya mazungumzo. Sasa huo ulikuwa migogoro mmoja, chukulia inapokuwa sita kama hiyo. Maana yake itachukua karibu miezi sita kutatua migogoro sita pekee. Binafsi naona uwekezaji ufanyike zaidi katika kuipima ardhi yote kwanza, kisha tuone aina mpya ya migogoro itakayozuka. Ardhi ikipimwa kila mmoja atajua kipande chake, baadaye utaandaliwa utaratibu wa kutoa hatimiliki kwa kila mwenye eneo na zisomeke popote ili kusiwe na mwanya wa kuzaliwa hati nyingine juu. Kuliko kutoa matamko ya kisiasa, ni vema kusoma mazingira kwanza, kisha kutafiti walipokwama watangulizi kisha kuja na mkakati mbadala utakaohakikisha unaleta angalau matunda. Kwa uhalisia unapopewa wizara nyeti kama ya ardhi, watu wanaangalia kujua utafanya nini cha tofauti, ni vema kuwa na malengo ya kutatua changamoto msingi ndiyo kuanza kusaka mengine yanayojitokeza baadaye. Kwa sababu migogoro ni zao la changamoto katika upimaji na upangaji wa ardhi, ni vema Serikali ianzie na hatua hii kisha mambo mengine yatajirekebisha yenyewe.
Rais Samia Suluhu Hassan amesema migogoro ya wakulima na wafugaji na athari za wanyama waharibifu wi
Rais Samia Suluhu Hassan amesema migogoro ya wakulima na wafugaji na athari za wanyama waharibifu wilayani Nachingwea ni miongoni mwa mambo yatakayoshughulikiwa na Serikali Kuu. Kauli hiyo ya Rais Samia imekuja baada ya hatua mbalimbali za Wilaya na Mkoa wa Lindi kushindwa kufua dafu juu ya changamoto hizo. Kero ya wanyama wakali na migogoro ya wakulima na wafugaji imeibuliwa na Mbunge wa Nchingwe, Amandus Chinguile aliyesema pamoja na juhudi mbalimbali kunahitajika hatua zaidi. “Kama sijasema kadhia ya ufugaji wananchi hawatanielewa na kura hizi nazitaka, lazima niseme walichonambia niseme. Tunajua kuwa nchini wapo wafugaji na wakulima, lakini katika maeneo yetu sisi ni wakulima, kuna mifugo mingi kwenye maeneo yetu inayoathiri mashamba yetu,” amesema. Rais Samia ameeleza hayo wilayani Nachingwea leo, Septembea 17, 2023 alipohutubia wananchi wa wilaya hiyo katika mwendelezo wa ziara zake. Katika hotuba yake hiyo iliyochukua dakika sita, ameeleza kusikitishwa na hatua ya wananchi 10 kuuawa na tembo kwa kipindi cha mwaka 2021 hadi 2023. “Nasikitishwa sana kwamba hapa Nachingwea kwamba kutoka 2021 hadi 2023 kiasi cha watu 10 wameshauawa na wanyama wakali hii si sura inayopendeza,” amesema. Ameeleza kwa kuwa inaonekana katika ngazi ya Wilaya na Mkoa limeshindikana, kikao cha kitaifa kitafanyima kushughulikia hilo, kadhalika na lile la migogoro ya wakulima na wafugaji. “Tunakwenda kulikomesha kadhia hii ya wakulima kuuawa kwa sababu ya wafugaji, kutoa umuhimu zaidi kwa uhai wa ng’ombe kuliko wa binadamu,” amesema. Awali, akizungumza katika mikutano huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohammed Mchengerwa amesema kila changamoto wizara husika zitashughulikia kwa maelekezo ya Rais Samia. “Sisi mawaziri wako vijana tutakwenda kukaa kwa pamoja kuona namna tunakavyoshughulikia matatizo haya kwa maelekezo yako,” amesema.
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi wilayani Liwale katika Mkoa wa Mtwara, kuacha tabia ya kuw
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi wilayani Liwale katika Mkoa wa Mtwara, kuacha tabia ya kuwaozesha watoto wa kike badala ya kuwapeleka shuleni. Rais Samia ameyasema hayo leo, Septemba 17, 2023 alipohutubia katika mikutano wa hadhara wilayani Liwale mkoani Lindi, ikiwa ni muendelezo wa ziara zake katika Mikoa ya Kusini. Amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya wazazi wilani humo, wanaamua kuwapangia watoto shughuli nyingine na kuacha kuwapeleka shule. “Watoto mnawaficha hawaendi kuripoti shuleni, mnawapangia kazi nyingine, mnawaozesha sasa hii haitatufikisha popote,” amesema. Ameeleza msingi wa mabadiliko ya wilaya hiyo ni uwepo wa wasomi wa kutosha na kwamba kupatikana kwao kutatokana na kupelekwa shuleni. Rais Samia ameeleza kusikitishwa na kitendo hicho, akifafanua Serikali imekuwa ikifanya kila namna kuboresha miundombinu ya elimu lakini baadhi ya wazazi wanaamua kutowapeleka watoto kusoma. Katika hatua nyingine, mkuu huyo wa nchi ameahidi kushughulikia changamoto ya upatikanaji wa huduma ya nishati ya umeme wilayani humo. “Tumepanga kuunganisha huduma za umeme katika Mikoa hii kutoka Gridi ya Mkoa wa Ruvuma,” amesema. Changamoto nyingine aliyoahidi kuishughulikia ni wanyama waharibifu, akisema kwa kuwa ngazi ya Wilaya na Mkoa wameshindwa, litachukuliwa kitaifa na kutatuliwa haraka.
Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imetangaza zabuni tatu za ujenzi wa bandari mbalimbali nchini ikiw
Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imetangaza zabuni tatu za ujenzi wa bandari mbalimbali nchini ikiwemo ya Kisiwa Mgao mkoani Mtwara, ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa maboresho ya bandari hizo. Zabuni nyingine zilizotangazwa ni ile inayohusisha uundaji na ujenzi wa bandari ya Mbegani wilayani Bagamoyo, kadhalika bandari ya Tanga. Zabuni hizo, zinatangazwa kipindi ambacho kumekuwa na hoja kutoka kwa baadhi ya wananchi, kwamba bandari zote nchini zimekabidhiwa kwa DP World. Msingi wa hoja hizo ni sehemu ya pili ya mkataba wa uwekezaji na uendelezaji wa bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia DP World, inayosema bandari zote zitakuwa chini ya kampuni hiyo. Katika tangazo la zabuni hiyo Septemba 8, mwaka huu TPA ilitangaza kusaka mkandarasi wa ujenzi wa bandari ya Mbegani Bagamoyo, huku ikieleza mwaliko wa mzabuni utatolewa Novemba mwaka huu. Kulingana na TPA katika tangazo hilo ililolitoa kwenye vyombo mbalimbali vya habari, waombaji wote wanapaswa kutuma nyaraka za maombi kwa lugha ya Kiingereza, baada ya kujisajili katika Mfumo wa Taifa wa Ugavi (Nest). “Maombi yote yatumwe kupitia Nest kabla ya saa 2:00 PM Septemba 9, mwaka huu na yatafunguliwa mara tu yatakapotumwa na muombaji ataona ripoti ya mwenendo wa maombi yake,” ilieleza sehemu ya tangazo hilo lenye anuani ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa. Lakini, zabuni hizo za TPA zinathibitisha ukweli wa kile ilichokuwa inakisisitiza tangu awali kwamba, mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uendelezaji wa bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai kupitia DP World hauhusishi bandari zote, ingawa wapo waliobuka kupinga. Akizungumza na Mwananchi, Mtaalamu wa mikataba ya kimataifa, Dk Rugelemeza Nshalla alieleza zabuni hizo katika pande mbili, akisema unaweza kuwa ujanja ujanja kwa upande mmoja, lakini yanaweza kuwa maamuzi ya kisheria ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA). Hoja ya ujanja ujanja aliijenga na kile alichokieleza, sehemu ya pili ya mkataba huo (IGA) imeweka wazi kwamba unahusisha bandari zote za Tanzania, iweje itangazwe zabuni kwa wengine. “Ni ujanja ujanja tu kwa sababu IGA imejieleza wazi, lakini hata agizo la Rais Samia ndani ya mkataba unaeleza bandari zote,” alisema Dk Nshalla. Kwa upande mwingine, nguli huyo wa sheria, alisema TPA inayo mamlaka ya kisheria ya kupuuzia mkataba huo, ingawa mamlaka hayo hayatakuwa na mashiko mbele ya jambo lililoamriwa na mkuu wa nchi na bunge limeliridhia. “Rais Samia na Mbarawa (Waziri wa Uchukuzi) walikosea, TPA ikiamua kusema inawapuuza ni sawa lakini tunaeleza maagizo ya mkubwa na bunge limeridhia kwamba bandari zote tumemkabidhi DP World,” alisema. Lakini, alisema hatua hiyo itazalisha mgogoro baina ya hao watakaopewa zabuni na TPA, ilhali kimkataba DP World inajua bandari hiyo ni ya kwake. Jambo hilo pia, limeibua mitazamo miwili ya Mkurugenzi wa Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA), Bob Wangwe aliyesema kwa upande mmoja kinachofanyika hakiendani na mwenendo wa makubaliano ambayo Tanzania na DP World wameingia. “Moja ya bandari iliyohusishwa katika mkataba husika ni hiyo ambayo TPA imetangaza tenda yake, watu wa TPA wana wajibu wa kuwaeleza Watanzania imekuwaje inatangaza tenda katika eneo ambalo Serikali yake na Bunge limeridhia ipewe DP World,” alisema. Lakini kwa upande mwingine, Wangwe alisema upo uwezekano wa kinachofanyika kuwa mbinu ya kisiasa katikati ya mambo ya kisheria ili kupeleka picha nyingine kwa umma. “Inawezekana hicho kilichofanyika kinalenga kujibu ile hoja ya bandari zote zinauzwa. Na kama kweli, nchi inajiingiza hatarini kwa sababu wale ilioingia nao mkataba (DP World) wakiamua kwenda mahakamani hatari inakuwa upande wetu (Tanzania),” alisema. Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mtaalamu wa Sheria, Profesa Issa Shivji pamoja na kukiri kuwa sehemu ya pili ya mkataba wa IGA umetoa bandari zote nchini, lakini alisema ni vigumu kulielezea hilo, kwa kuwa haijulikani mikataba mengine iliyopo. “Siwezi kujua, sehemu ya pili ya IGA ambao ni mkataba mama inaeleza kuwa mkataba unahusu bandari zote, sasa kama kuna tenda imetangazwa siwezi kujua uhalali wake. “Kwa sababu ndani ya mkataba mama kunaweza kuwa na mikataba mengine ambayo siijui wenyewe (TPA) ndiyo waseme,” alisema. Alipotafutwa kuzungumzia zabuni hizo, Mbossa alisema sio bandari hizo pekee, zabuni inatarajiwa kutangazwa katika bandari nyingine kadhaa. “Kilichopo, Serikali imekuwa ikisema bandari zote kutolewa si tafsiri sahihi ya mkataba, ule ni mkataba wa ushirikiano kati ya Tanzania na Dubai katika kuendeleza bandari za Tanzania. “Serikali ilitoa ufafanuzi lakini watu waliokuwa na malengo tofauti waliendelea kuwaaminisha watu kinyume,” alisema. Alieleza mkataba wa IGA haumpi mwekezaji sehemu yoyote kisheria, bali unafugua milango ya majadiliano juu ya mikataba ya Uwekezaji (HGA) na ile ya utekelezaji. Kuhusu zabuni hizo, alisisitiza “tunataka sasa ule mradi mkubwa wa kujenga bandari ya Bagamoyo ndiyo tumeanza hivi, tulishaweka katika bajeti lengo ni kuhakikisha ukuaji wa shughuli za kiuchumi unakutana na bandari ya kisasa kabisa yenye uwezo wa kupokea meli kubwa.” Nyingine ambazo tenda zake zitatangazwa, alisema ni Mbambabay, Kimondo na Bukoba, Mwanza, Tanga na Dar es Salaam watasaini mkataba wa kujenga kituo kikubwa cha kupokea mafuta. Lakini, alisisitiza kitakachofanywa na DP World ni kama kile ambacho TICTS ilipewa kufanya. “Wananchi waelewe tu kwamba sio rahisi Serikali iwadanganye,” alisema.
Katika kila wanafunzi 10 wa sekondari waliofanya mtihani wa hesabu kwa kipindi cha miaka mitano ni w
Katika kila wanafunzi 10 wa sekondari waliofanya mtihani wa hesabu kwa kipindi cha miaka mitano ni wawili pekee ndiyo waliofaulu. Hii ni sawa na kusema ni asilimia 20 pekee ya wanafunzi wa sekondari wanaofanya mtihani wa hesabu wanafaulu, huku asilimia 80 wakifeli. Kulingana na Chama cha Hisabati Tanzania (CHAHITA), mrundikano wa vipindi bila walimu wa kutosha wa hesabu na adhabu kali kutoka kwa baadhi ya walimu wa masomo hayo ni miongoni mwa sababu za ufaulu duni. Lakini, ufaulu duni wa somo la hisabati ni kitendawili cha muda mrefu kilichokosa jawabu, huku kila siku zikiibuka sababu mpya za hali hiyo. Anguko la ufaulu katika somo hilo, ndiyo sababu ya kuonekana haja ya kuundwa kwa Chahita mwaka 1966, kikilenga kujua mzizi wa changamoto hiyo. Katika mahojiano yake na gazeti hili, Mwenyekiti wa Chahita, Betinasia Manyama anasema mrundikano wa wanafunzi darasani na unaosababisha mzigo kwa walimu wa somo hilo ni miongoni mwa mzizi wa tatizo. “Idadi ya vipindi inakuwa kubwa zaidi na mwalimu anashinda kumudu kuwafundisha wanafunzi wote somo la hisabati kwa makini zaidi,” alisema. Uchache wa walimu ni changamoto nyingine iliyotajwa na Betinasia kuwa sababu ya ufaulu duni wa wanafunzi, akifafanua wengi wamestaafu na waliopo aghalabu huhamishwa vitu vya kazi. "Tunaomba Serikali ituangalie kwa jicho la pekee, tupo wachache na tunaelemewa tunaomba tuongezewe walimu. Imekuwa changamoto na tunashindwa kutoa hata motisha kwa wanafunzi kutokana na uchache uliopo," anasema. Ombi lake hilo, aliliambatanisha na haja ya kutolewa motisha kwa walimu wa hisabati ikiwemo kuongezewa posho na mishahara ili kuwapa hamasa. “Unakuta mwalimu mmoja ana vipindi 30 huku kwa walimu wa masomo mengine wana vipindi hadi nane,” anasema. Anguko la wanafunzi katika somo hilo, wakati mwingine Betinasia anasema linachagizwa na ukali wa baadhi ya walimu wa hisabati, ambao aghalabu huingia darasani na rundo la viboko. "Tunaomba walimu wa somo la hisabati wapunguze tabia ya ukali na kuingia na viboko darasani. Hii inawachanganya wanafunzi tujitahidi kuongeza bidii na mbinu katika ufundishaji,” anasema. Kulingana na Betinasia, wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa fedha kuwawezesha walimu kutembelea shule mbalimbali kuwahamasisha wanafunzi kupenda somo hilo. Lakini, hata yakiandaliwa mafunzo na Chahita, anasema walimu wanaohudhuria ni wachache. Baada ya chama hicho kuanzishwa, anasema mikakati iliwekwa ikiwemo kuanzisha semina kwa walimu inayofanyika mara moja kila mwaka ili kuwapa mbinu bora za ufundishaji. Pamoja na mbinu bora za kufundishia, uwezo wa kufanya utafiti ni jambo lingine alilosema linafanywa katika semina hizo kwa walimu. "Kupitia semina hizo tumekuwa tukiwandaa walimu katika kufanya tafiti mbalimbali darasani pamoja na kuziandika ili somo la hesabu liendee,” anasema. Katika utekelezaji wa majukumu yake, anasema chama hicho kwa sasa kimeshatembelea shule zaidi ya 20 ili kuhamasisha wanafunzi kupenda somo hilo. "Walimu wanajitolea kwa nauli zao kwenda kuhamasisha katika baadhi ya shule kuhusu somo la hisabati na tayari tuna shule zaidi ya 20 tumeshazitembelea,” alisema. Ushirikiano na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika kufanya tafiti za kubaini changamoto ni miongoni mwa mafanikio ya chama hicho. Katika maelezo yake hayo, Betinasia anasema kuna umuhimu wa mwanafunzi kujua hesabu kwa kuwa ndiyo msingi bora wa maisha, akisistiza kwenye kila eneo inatumika. Kuhusu maboresho ya sera na mitalaa yanayoendelea, anaeleza kukoshwa na muendelezo wa kulifanya somo la hesabu kuwa la lazima. "Mitaala inayoandaliwa ni mizuri hivyo tunaomba wanaosimamia waweke mikakati mizuri, pia wazingatie uwepo wa vifaa vya kutosha katika kufundishia hususani vitendea kazi kwa ujumla,” anasema. Anasisitiza uwiano wa walimu wa hesabu na wanafunzi uzingatiwe ili kupunguza mzigo kwa wataalamu hao. "Unakuta kwenye shule za halmashauri nyingi walimu ni wachache lakini wanafunzi ni wengi sana, kwa mfano unakuta mwalimu wa kiswahili ana vipindi nane tu huku wa hesabu akiwa na vipindi 30. “Ni vigumu sana kwa mwalimu huyu kumudu hilo, tunaomba Serikali iongeze miundombinu rafiki kwa walimu wa somo la hisabati ili wafanye vizuri zaidi," anasema. Kuimarishwa kwa klabu za hisabati ni miongoni mwa mambo yaliyotajwa kuleta ahueni ya changamoto kama inavyoelezwa na Ofisa elimu sekondari mkoa wa Arusha, Abel Ntupwa. Pamoja na uimarishwaji klabu hizo, Ntupwa anawataka walimu hao kuacha kujilimbikizia mikopo kutoka taasisi mbalimbali, kwa kuwa inawasababishia msongo wa mawazo na kupunguza maarifa. “Mikopo hii inapunguza maarifa, kwa sababu mnaingia darasani mkiwa na mawazo, hii inawasababisha mshindwe kushirikiana vema na wanafunzi,” anasema. Mabadiliko ya mtazamo wa walimu kutoka kufundisha kwa mazoea hadi kubuni mbinu mpya, anayataja kuwa muarobaini mwingine utakaoongeza ufaulu wa somo hilo. "Nawaombeni sana muwe na ujasiri na kuthubutu, tumieni ndoto mlizonazo ili tuwe msaada kwa jamii, familia na nchi kwa ujumla na tuhakikishe tunaacha tabia za kufedhehesha somo la hisabati bali tutafute namna ya kutoka ili chama hiki kiwe mfano wa kuigwa," anasema. Katika maelezo yake, anairejea hoja ya Betinasia ya kuongeza fedha kwa ajili ya walimu wa somo la hisabati kwa kuwa wanafanya kazi inahitaji motisha ili kuwaongezea ari. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Dk Cairo Mwaitete anasema fani ya mahesabu ni muhimu kwenye kila idara kwani inatumika kila mahali. Anasema hata wahasibu hutumia hesabu katika shughuli zao, hivyo ni muhimu kutoa motisha kwa wanafunzi kulipenda somo hilo kwa kuwa lina soko pana la ajira. "Sisi chuo cha uhasibu fani zetu tunazingatia mahesabu zaidi, ni vizuri tukatambua kuwa hesabu ni msingi wa maendeleo kwa faida ya nchi yetu na ni somo linalopaswa kuzingatiwa kuanzia shule za msingi hadi vyuoni," anasema.
Katikati ya hoja kuwa bandari zote nchini imeuziwa kampuni ya DP World, Mamlaka ya Bandari Tanzania
Katikati ya hoja kuwa bandari zote nchini imeuziwa kampuni ya DP World, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imetangaza zabuni za ujenzi wa bandari zake mbalimbali ikiwemo ya Mbegani Bagamoyo. Hatua hiyo ya TPA kutangaza zabuni hizo, inathibitisha ukweli wa kile ilichokuwa inakisisitiza tangu awali kwamba, mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uendelezaji wa bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai kupitia DP World hauhusishi bandari zote. Wakati hatua hiyo ikitazamwa kama ithibati ya maelezo ya Serikali, baadhi ya wadau wameonyesha wasiwasi wa zabuni hizo wakizihusisha na jangajanga na mbinu ya kisiasa ya mamlaka kutaka kuuaminisha umma kuwa, bandari hazijatolewa kwa DP World. Msingi wa hoja ya bandari zote zimekabidhiwa kwa DP World, unatokana na sehemu ya pili ya mkataba wa IGA, ambayo kulingana na wataalamu wa sheria, imeweka bayana kuwa bandari zote zitakuwa chini ya kampuni hiyo kutoka Dubai. “Siwezi kujua, sehemu ya pili ya IGA ambao ni mkataba mama inaeleza kuwa mkataba unahusu bandari zote, sasa kama kuna tenda imetangazwa siwezi kujua uhalali wake,” alisema Profesa Issa Shivji, mtaalamu wa sheria. Akizungumza na Mwananchi, Mtaalamu wa mikataba ya kimataifa, Dk Rugelemeza Nshalla alieleza kinachoendelea katika pande mbili, akisema unaweza kuwa ujanja ujanja kwa upande mmoja, lakini yanaweza kuwa maamuzi ya kisheria ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA). Hoja ya ujanja ujanja aliijenga na kile alichokieleza, sehemu ya pili ya mkataba huo (IGA) imeweka wazi kwamba unahusisha bandari zote za Tanzania, iweje itangazwe zabuni kwa wengine. “Ni ujanja ujanja tu kwa sababu IGA imejieleza wazi, lakini hata agizo la Rais Samia ndani ya mkataba unaeleza bandari zote,” alisema Dk Nshalla. Kwa upande mwingine, nguli huyo wa sheria, alisema TPA inayo mamlaka ya kisheria ya kupuuzia mkataba huo, ingawa mamlaka hayo hayatakuwa na mashiko mbele ya jambo lililoamriwa na mkuu wa nchi na bunge limeliridhia. “Rais Samia na Mbarawa (Waziri wa Uchukuzi) walikosea, TPA ikiamua kusema inawapuuza ni sawa lakini tunaeleza maagizo ya mkubwa na bunge limeridhia kwamba bandari zote tumemkabidhi DP World,” alisema. Lakini, alisema hatua hiyo itazalisha mgogoro baina ya hao watakaopewa zabuni na TPA, ilhali kimkataba DP World inajua bandari hiyo ni ya kwake. Jambo hilo pia, limeibua mitazamo miwili ya Mkurugenzi wa Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA), Bob Wangwe aliyesema kwa upande mmoja kinachofanyika hakiendani na mwenendo wa makubaliano ambayo Tanzania na DP World wameingia. “Moja ya bandari iliyohusishwa katika mkataba husika ni hiyo ambayo TPA imetangaza tenda yake, watu wa TPA wana wajibu wa kuwaeleza Watanzania imekuwaje inatangaza tenda katika eneo ambalo Serikali yake na Bunge limeridhia ipewe DP World,” alisema. Lakini kwa upande mwingine, Wangwe alisema upo uwezekano wa kinachofanyika kuwa mbinu ya kisiasa katikati ya mambo ya kisheria ili kupeleka picha nyingine kwa umma. “Inawezekana hicho kilichofanyika kinalenga kujibu ile hoja ya bandari zote zinauzwa. Na kama kweli, nchi inajiingiza hatarini kwa sababu wale ilioingia nao mkataba (DP World) wakiamua kwenda mahakamani hatari inakuwa upande wetu (Tanzania),” alisema. Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mtaalamu wa Sheria, Profesa Issa Shivji pamoja na kukiri kuwa sehemu ya pili ya mkataba wa IGA umetoa bandari zote nchini, lakini alisema ni vigumu kulielezea hilo, kwa kuwa haijulikani mikataba mengine iliyopo. “Siwezi kujua, sehemu ya pili ya IGA ambao ni mkataba mama inaeleza kuwa mkataba unahusu bandari zote, sasa kama kuna tenda imetangazwa siwezi kujua uhalali wake. “Kwa sababu ndani ya mkataba mama kunaweza kuwa na mikataba mengine ambayo siijui wenyewe (TPA) ndiyo waseme,” alisema. Naibu Katibu Mkuu Chadema, Salum Mwalimu alisema kwa kuwa Serikali imesema IGA haihusishi bandari zote na kwa kutoa tenda katika moja ya bandari zake hana la kuzungumza zaidi. “Labda waulizwe DP World watuambie kama ipo sawa, lakini siwezi kuingia kichwa kichwa nikapiga siasa kwenye jambo lenye mantiki kama hili,” alisema. Alipotafutwa kuzungumzia zabuni hizo, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa alisema sio bandari hizo pekee, zabuni inatarajiwa kutangazwa katika bandari nyingine kadhaa. “Kilichopo, Serikali imekuwa ikisema bandari zote kutolewa si tafsiri sahihi ya mkataba, ule ni mkataba wa ushirikiano kati ya Tanzania na Dubai katika kuendeleza bandari za Tanzania. “Serikali ilitoa ufafanuzi lakini watu waliokuwa na malengo tofauti waliendelea kuwaaminisha watu kinyume,” alisema. Alieleza mkataba wa IGA haumpi mwekezaji sehemu yoyote kisheria, bali unafugua milango ya majadiliano juu ya mikataba ya Uwekezaji (HGA) na ile ya utekelezaji. Kuhusu zabuni hizo, alisisitiza “tunataka sasa ule mradi mkubwa wa kujenga bandari ya Bagamoyo ndiyo tumeanza hivi, tulishaweka katika bajeti lengo ni kuhakikisha ukuaji wa shughuli za kiuchumi unakutana na bandari ya kisasa kabisa yenye uwezo wa kupokea meli kubwa.” Nyingine ambazo tenda zake zitatangazwa, alisema ni Mbambabay, Kimondo na Bukoba, Mwanza, Tanga na Dar es Salaam watasaini mkataba wa kujenga kituo kikubwa cha kupokea mafuta. Lakini, alisisitiza kitakachofanywa na DP World ni kama kile ambacho TICTS ilipewa kufanya. “Wananchi waelewe tu kwamba sio rahisi Serikali iwadanganye,” alisema.
Bado safari ya miaka 30 ya demokrasia nchini, haijafua dafu katika kuleta chachu ya ushiriki wa wana
Bado safari ya miaka 30 ya demokrasia nchini, haijafua dafu katika kuleta chachu ya ushiriki wa wanawake kwenye ushindani wa kisiasa majimboni. Hilo linathibitishwa na kile kilichoelezwa na wadau wa demokrasia nchini, tangu kuanza kwa mfumo wa siasa za vyama vingi ni asilimia 9.4 pekee ya wanawake ndiyo walioshinda ubunge kwa kuchaguliwa. Hiyo ni sawa na kusema, itahitaji subira ya miaka 120 ijayo ili angalau Tanzania iwe na asilimia 50 ya wabunge wanawake waliotokana na kuchaguliwa majimboni. Hayo yaliibuliwa jijini Dar es Salaam jana na Mhadhiri wa Sheria kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), Dk Victoria Lihiru katika hafla ya maadhimisho ya miaka 30 ya demokrasia, ulioandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Katika Bunge la sasa, Dk Victoria alisema kati ya wabunge 264 kutokea majimboni 26 pekee ndiyo wanawake, sawa na asilimia 9.4. Ingawa idadi hiyo ni ongezeko kutoka wabunge wanane wanawake walioshinda katika uchaguzi wa mwaka 1995, alisema bado kuna safari ndefu. "Kumekuwa na idadi ndogo ya ongezeko la wanawake wanaoshinda katika uchaguzi wa wabunge, kila mwaka ni asilimia tatu pekee. "Kama imechukua miaka 30 kupata asilimia 9.4 ya wabunge wanawake waliochaguliwa majimboni, maana yake itachukua miaka mingine mingi zaidi kupata asilimia 50," alisema. Kulingana na Dk Victoria, hali hiyo inachagizwa na sababu za kisheria, kijamii na mambo mengine. Miongoni mwa sababu hizo, alieleza ni mifumo yenyewe ya uchaguzi hasa kile kipengele cha wingi wa kura ndiyo kigezo cha ushindi. "Huu mfumo unatuonyesha kwamba kila mtu anaweza akasimama akateuliwa akapigiwa kura. Mfumo unasahau mila na tamaduni zilizoweka makundi fulani pembeni," alisema. Lakini, alieleza mfumo huo hauvipi chachu vyama kuteuwa wagombea wanawake wala wananchi kupata hamasa ya kuwachagua wanawake kwa kuwa hawajazoea kuongozwa nao. Alisema kuna haja ya kuwa na mfumo unaoweka pembeni mtazamo huo. Kwa upande mwingine, Dk Victoria alieleza uwepo wa mafanikio kadhaa katika safari ya miaka 30 ya demokrasia, ikiwemo ongezeko hilo la wanawake katika siasa. Alieleza mabadiliko mbalimbali ya sheria yalifanyika ikiwemo ile ya gharama za uchaguzi ili kuwaondoa hofu wanawake kushiriki. "Mafanikio mengine ni kupata Makamu wa Rais mwanamke, baadaye Rais mwanamke na Naibu Spika na baadaye Maspika wa Bunge," alisema. Lakini, safari ya miaka 30 ya demokrasia iligubikwa na milima na mabonde kwa asasi za kiraia kama anavyofafanua, Anna Henga Mkurugenzi wa LHRC. Ukiachana na wagombea wa vyama vya upinzani kuenguliwa katika uchaguzi wa mwaka 2020, Henga alisema hata waangalizi wa uchaguzi ambazo ni asasi za kiraia zilikumbwa na hilo. Alieleza katika kipindi hicho (miaka 30) kumekuwepo na changamoto ya usalama kwa waangalizi na wapo waliowahi kukamatwa. Changamoto nyingine, alisema ni asasi za kiraia kuhusishwa na vyama vya upinzani, ilhali mara zote haziegemei upande wowote. "Hatuegemei upande wowote labda kwa sababu tu vyama vya upinzani pengine vimekuwa vikikumbana na changamoto na tunaposimama kuvitetea ndiyo tunaonekana hivyo, lakini kiuhalisia hatuna upande," alisema. Hilo lilimuibua mwanasiasa mkongwe, Stephen Wassira aliyesema ni muhimu asasi za kiraia ziwe huru dhidi ya wananchi wote. Lakini, alisema asasi hizo zimefanya kazi kubwa katika miaka 30 ya demokrasia, ikiwemo kushinikiza mabadiliko mbalimbali hasa ya kisheria. Akichangia moja ya jopo katika mjadala huo, Katibu Mkuu wa Chadema, John Manyika alisema ili kupata tija ya mabadiliko mbalimbali yanayofanywa na Serikali ni muhimu vitu vya msingi vizingatiwe. Kulingana na Mnyika, katika miswada ya mabadiliko ya sheria tatu inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni Oktoba, ni muhimu iongezwe mingine ili iwe saba. Miswada inayowasilishwa Oktoba ni ya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi, sheria ya tume ya taifa ya uchaguzi na ile ya vyama vya siasa. Alisema pamoja na hiyo, kunapaswa kupalekwa miswada mingine ya sheria nne ambayo ni mabadiliko ya Katiba, mabadiliko madogo ya Katiba ya mwaka 1977 katika maeneo ya uchaguzi, sheria ya jeshi la Polisi na sheria ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Mabadiliko madogo ya Katiba, alisema yanalenga kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Mkuu wa 2025 inafanyika katika mazingira huru. Katika hafla hiyo, Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe alisema ni muhimu mabadiliko yatakayofanyika yahusishe sheria nne ikiwemo Katiba yenyewe. Lakini pamoja na Katiba, alisema yafanyike mabadiliko ya baadhi ya sheria kuruhusu kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika mazingira huru.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura), kuwapa zabu
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura), kuwapa zabuni wahandisi wazawa katika miradi ya ujenzi wa barabara ili kuongeza ufanisi wao. Hatua hiyo, Majaliwa amesema itaimarisha uwezo wa wahandisi wa Tanzania kusimamia miradi na kadri watakavyoimarika, Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) nayo itawapa zabuni. Maelekezo ya Majaliwa yalitokana na kauli ya Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wakandatasi, Wakili Menye Manga aliyesema bado kuna ushiriki mdogo wa wahandisi wa ndani katika miradi nchini. Majaliwa alitoa maelekezo hayo jijini Dar es Salaam jana, alipohutubia ufunguzi wa mkutano wa 20 wa maadhimishi ya siku ya Wahandisi nchini. "Tarura mnapaswa kuanza kuwapa wahandisi wa Tanzania kazi ya ujenzi wa barabara kilometa chache na baadaye watahamia kwenye zile kubwa, hili litawezekana hebu tuanze," alisema. Pamoja na hayo, Majaliwa aliitaka ufanisi wa wahandisi wa Tanzania wanapoaminiwa kutekeleza mradi. Alisisitiza kauli yake hiyo akitolea mfano mmoja wa miradi waliyopewa Watanzania ambao baadaye waliishia kusambaratika. "Wameanza vizuri kazi lakini baadae wakasambaratika na ukiangalia nini kimewasambaratisha ni yale malipo ya awali," alisema. Kitendo kama hicho, Majaliwa alisema kinaashiria uwezo duni wa wahandisi wa Tanzania katika kusimamia miradi, akisisitiza wanapaswa kubadilika. Katika hotuba yake hiyo, aliitaka Wizara ya Ujenzi kuongeza ushiriki wa Watanzania katika miradi inayoendelea. Aliitaka ERB kujifunze kutoka sekta ya madini na nishati kwa kupeleka mapendekezo yatakayowafanya Watanzania wawe na uwezo wa kutekeleza miradi wenyewe. Alitaka wahandisi wanawake waandaliwe mafunzo ya kuendelezwa, lakini Wizara ya Ujenzi inapaswa kutenga fedha kuwaendeleza wahandisi wahitimu. Akizungumza katika hafka hiyo, Wakili Manga alisema ushiriki wa wahandisi wa Tanzania pamoja na kampuni zao katika miradi nchini ni mdogo. Kinachoshangaza, alisema baadhi ya miradi zinapaswa kampuni za nje ya nchi zenye mazingira yanayofanana na Tanzania. Lakini, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuongeza ufanisi wa wahandisi nchini ili waendelee kuaminiwa na kutumiwa katika miradi nchini. "Mikakati ya kufikia shabaha hiyo ni kuongeza ujuzi wa kitaaluma na tunaendelea kufanya hivyo," alisema. Kuhusu mkutano huo, alisema matarajio ni kutoka na maazimio yatakayowasilishwa serikalini kwa ajili ya kufanyiwa kazi. "Tutakuwa na mabadiliko katika sheria na kanuni zetu ili kuongeza usajili zaidi wa wahandisi," alisema. Lakini, katika hafla hiyo, alisema wahandisi 200 wataapa kufanya kazi kwa weledi, nidhamu na kuzingatia maadili ya kazi ya uhandisi. "Kiapo watakachokula leo ni cha maisha anaapa kutekeleza majukumu yake ya kihandisi kwa maadili miaka yote," alisema. Hata hivyo, alisema vyuo vya Tanzania kwa sasa vinazalisha Wahandisi 3,500 wanaozingua katika soko la ajira kila mwaka na kwamba mpango wa mafunzo tarajali utaandaliwa kwa ajili ya kuwaendeleza. Naibu Waziri wa Ujenzi, Godfrey Kasekenya alisema Tanzania ina wahandisi 36,709 kati yao wanawake ni 4,653 sawa na asilimia 13. Alisema kunahitajika kuwa na wahandisi wengi zaidi na mafundi sanifu. Kwa kutambua shughuli za kihandisi, alisema katika mwaka wa fedha 2002/03 Serikali ilianzisha programu ya kuwashikiza wahandisi wahitimu kwenye miradi. Kila mwaka wizara ya ujenzi hutenga fedha kwa ajili ya hilo.
Ili kuiepushia Serikali hasara ya kulipa fidia kwa makosa mbalimbali ya kisheria, Waziri wa Katiba n
Ili kuiepushia Serikali hasara ya kulipa fidia kwa makosa mbalimbali ya kisheria, Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Pindi Chana ameitaka Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kutoa elimu kwa taasisi za umma na halmashauri nchini. Elimu hiyo, amesema inapaswa kulenga taratibu zinazopaswa kufuatwa wakati wa kuvunja mikataba iliyoingiwa kati ya taasisi au halmashauri na kampuni binafsi. Kauli hiyo ya Balozi Chana, inatokana na hoja iliyoibuliwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Dk Boniphace Luhende aliyesema kuvunjwa kwa mikataba pasi ya ofisi yake kushirikishwa ni moja ya changamoto inayoikabili ofisi hiyo. Dk Luhende alisema utaratibu huo wa kuvunjwa mikataba, aghalabu huchagiza migogoro lukuki ya madai ya fidia kwa taasisi za Serikali na wakati mwingine kusababisha hasara. Balozi Chana aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na menejimenti ya ofisi ya wakili mkuu wa Serikali, baada ya kuwasili katika ofisi hiyo kwa ajili ya kujitambulisha. Pamoja na kuitaka ofisi hiyo kuwa tayari kupokea taasisi zote za umma na kuzishauri, kadhalika aliielekeza kutoa elimu juu ya taratibu za kisheria wakati wa kuvunja mikataba na kampuni binafsi. "Halmashauri, Wizara na taasisi zetu zifanye kazi vizuri, kusiwe na upoteaji wa fedha eti kwa sababu ya kutofuatwa taratibu fulani," alisema. Aliisisitiza hoja yake hiyo na kile alichoeleza ni jukumu la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kuhakikisha inalinda maslahi ya Serikali katika masuala mbalimbali. Msingi wa maelekezo ya Balozi Chana ni kile kilichoelezwa awali na Dk Luhende alipotoa taarifa kwa Waziri huyo, akisema baadhi ya taasisi za umma huvunja mikataba au makubaliano ziliyoingia na kampuni binafsi bila kuihusisha ofisi yake. Jambo hilo, alisema haliishii kuwa mgogoro, mara nyingi hufikia hatua ya kuisababisha hasara kwa Serikali kwa kutozwa fidia. Alizitaja changamoto nyingine zinazoikabili ofisi yake ni baadhi ya taasisi za umma kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi pasi na kuzingatia sheria. Alieleza hatua hiyo inasababisha kuzaliwa kwa utitiri wa migogoro ya ajira. Usimamizi hafifu wa miradi hasa ya ujenzi, ni changamoto nyingine iliyotajwa na Dk Luhende inayosababisba migogoro mingi hasa ya usuluhishi. Lakini, alisema zipo baadhi ya taasisi za Serikali zinachelewesha malipo ya huduma kwa wakandatasi na kusababisha mashauri mengi ya madai ya fidia. Kwa mujibu wa Dk Luhende, ofisi hiyo pia inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi wabobevu wa kuendesha mashauri ya migogoro hasa ya Kimataifa na mashauriano katika eneo la mafuta na gesi. Pamoja na uwepo wa changamoto hizo, alisema mafanikio lukuki yamepatikana ikiwemo kumaliza baadhi ya mashauri nje ya mahakama.
Rais Samia Suluhu Hassan ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Kituo cha Dunia cha Uhimilivu
Rais Samia Suluhu Hassan ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Kituo cha Dunia cha Uhimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCA). Hatua hiyo inamfanya Rais Samia kuwa mkuu wa nchi wa pili ndani ya bodi hiyo inayojumuisha wajumbe watano, akiwemo Rais wa Senegal, Macky Shall. Mbali na marais hao, wajumbe wengine katika bodi hiyo ni Moussa Mahmat ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Akinumwi Adesina na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Kristalina Georgieva. Hata hivyo, nafasi hiyo inamfanya Rais Samia kuwa na nguvu ya kupeleka hoja moja kwa moja kuzishinikiza nchi zilizoendelea zitekeleze ahadi ya kutoa fedha za uhilimivu wa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi zinazoendelea kama inavyoelezwa na wadau. Taarifa ya uteuzi huo, imetolewa na Mwenyekiti wa bodi hiyo, Ban Ki-Moon walipokutana na Rais Samia katika mikutano wa wakuu wa nchi kuhusu mabadiliko ya tabianchi, uliofanyika Nairobi nchini Kenya. Akizungumza na Mwananchi Digital leo Septemba 12, 2023 Meneja wa Mipango wa Shirika la linalojishughulisha na athari za mabadiliko ya tabianchi (ForumCC), Msololo Onditi amesema uteuzi huo ni tija kwa Tanzania. Tija hiyo inatokana na kile alichoeleza, mkuu huyo wa nchi atakuwa na nguvu ya kuwasilisha moja kwa moja hoja za kuzishinikiza nchi zilizoendelea kutoa fedha za kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi. “Kwa nafasi hiyo atakuwa na sauti ya kupaza kwa nchi zilizoendelea kutoa fedha za uhimili wa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi zinazoendelea kama zilivyoahidi,” amesema. Lakini wadhifa huo, Onditi amesema unaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zitakazokuwa na fursa ya kupata taarifa ya fedha za mabadiliko ya tabianchi haraka na kujiandaa kuzipokea. “Kwa sababu Rais Samia anakuwa mjumbe maana yake tutapata taarifa za haraka na kujiandaa kuzipokea, tofauti na nyakati nyingine, huwa tunakuwa nyuma ya mipango,” amesema. Onditi amesema GCA pamoja na mambo mengine, hujihusisha na kushauri juhudi za uhimilivu wa athari za mabadiliko ya tabianchi na husaidia mazungumzo na nchi zilizoendelea kufanikisha upatikana wa fedha.
Katika kipindi cha mwaka 1994 hadi 2019, zaidi ya Sh9 bilioni zimetumika kulipa madeni ya bima kwa w
Katika kipindi cha mwaka 1994 hadi 2019, zaidi ya Sh9 bilioni zimetumika kulipa madeni ya bima kwa wanachama mbalimbali wa NiC Insurance. Malipo hayo ni yale ya wanachama walioshindwa kulipwa kwa wakati, kutokana na changamoto zilizokuwa zikilikabili shirika hilo. Kulingana na Mkurugenzi wa shirika hilo, Dk Elirehema Doriye, katika kipindi cha miaka 55 tangu kuanzishwa kwake 1963 hadi 2019, halikuwa likizalisha faida. Dk Doriye aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana, alipotoa mafanikio ya NiC katika kipindi cha mwaka 2019/2020-2021/22 mbele ya wahariri na waandishi wa habari. Alisema mchakato wa mabadiliko ya shirika hilo, umewezesha malipo ya madai ya bima za maisha zaidi ya Sh9 bilioni ambayo awali yalishindikana kulipwa. "Kwa sababu Shirika lilikuwa katika kipindi kigumu kwa muda mrefu, kwenye bima za maisha tuliamua kurudi kuanzia mwaka 1994. "Hii ililenga kuhakikisha kila mteja anayetudai na hadi sasa hakuna mteja anayetudai kuanzia mwaka huo hadi sasa, tumelipa zaidi ya Sh9 bilioni," alisema. Alieleza mbinu zilizotumika kuwapata wadai hao ni kukutana na maofisa utumishi wa ofisi mbalimbali ili kujua walipo wafanyakazi hao. Hatua hiyo, alisema umewezesha kuwapata wateja hao na michakato inafanyika kwa ajili ya malipo. Hata hivyo, Dk Doriye alisema hali mbaya ya shirika hilo nyuma ya mwaka 2019, ilisababishwa na uwepo wa watu wengi waliokuwa wanadai, ingawa baada ya uchambuzi baadhi yalionekana kuwa hewa. Hali hiyo, kulingana na Dk Doriye yalisababisha haja ya kufanyika mabadiliko iliyoanzia katika uongozi na ndiyo yaliyomuingiza katika nafasi hiyo ya ukurugenzi. Mabadiliko ya uongozi, alisema yaliambatana na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi. "Hii ilihusisha kuondoa maeneo yanayovujisha mapato au yanasababisha shirika lisipate faida," alisema. Mabadiliko mengine, Dk Doriye alisema ni weledi wa kuhakikisha kila mfanyakazi anafanya shughuli zake kwa ubora na kuwa msingi wa mafanikio ya shirika. "Tuliangalia kwa kiwango gani kila mfanyakazi atachangia maendeleo ya NiC, kuanzia mfanyakazi wa chini hadi wa juu kila mmoja tulihakikisha tunajua mchango wake ni nini," alisema. Uwekezaji katika rasilimali watu ni mabadiliko mengine aliyosema yamefanyika kuhakikisha kunakuwa na wataalamu. "Ili kupata tija, ililazimu kuwekeza kwa kiasi kikubwa kwenye wafanyakazi, tuliongeza wafanyakazi kutoka Taasisi nyingine Kati ya asilimia 25 hadi 30," alisema Kulingana na Dk Doriye, mpango mkakati wa shirika hilo ilibadilisha kuliwezesha kufanya biashara badala ya kutoa huduma kama ilivyo kwa mengine mengi ya Serikali. "Tulileta mabadiliko kwenye tafsiri ya utendaji kazi na nini na kwa namna gani tunavyopaswa kufanya, tulipitia upya, dira, dhima na misingi, zote tulizibadilisha ili ziendane na uhalisia wa biashara tunayofanya," alisema. Alisema mpango mkakati wao uliakisi kuwa shirika hilo ni la kibiashara. Mabadiliko hayo, alisema yalisababisha mtazamo mpya na ukaanza kujengwa kwa wafanyakazi ili watoe huduma kibiashara. Maboresho mengine, alisema ni uwekezaji wa mifumo ya Tehama karibu asilimia 90, akisema kabla ya mwaka 1999 uendeshaji wa shughuli ulikuwa kwa karatasi. Mwaka 2019, alisema ulipaji wa madai ulichukua siku 35 hadi 45 lakini sasa ni siku saba, ikiwa ni matokeo ya mabadiliko. "Ukiwasilisha madai yako na nyaraka tunakulipa ndani ya siku saba na zinaweza kupungua," alisema. Miongoni mwa kazi ngumu katika safari hiyo, Dk Doriye alisema ni kurudisha imani ya wateja hali ambayo ilichagiza kubadilishwa kwa muonekano wa shirika. Alisema maboresho hayo yameleta tija kwa shirika hilo, hadi kutambuliwa na kupewa chapa ya Superbrand Afrika Mashariki. Tija nyingine zilizopatikana, alisema ni faida katika shirika hilo, akifafanua mwaka 2020 Sh33.6 bilioni, 2021 Sh63.5 bilioni na mwaka 2022 Sh63 bilioni. "Kabla ya hapo shirika halikuwa linapatw faida, lilikuwa moja ya mashirika yaliyokuwa katika hatihati ya kufutwa, kwa kuwa Serikali iliwekeza sana lakini haikupata tija yake," alisema. Alisema kwa sasa NiC inatoa gawio na mwaka 2022 ilitoa Sh2 bilioni Kulingana na Dk Doriye, mabadiliko yaliyofanyika yamesababisha shirika hilo likue kwa asilimia 108, likimiliki soko kwa asilimia 16 hadi Desemba mwaka jana.
Unajua tangu ruhusa ya mikutano ya hadhara, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimefanya zi
Unajua tangu ruhusa ya mikutano ya hadhara, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimefanya ziara nyingi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ukilinganisha na kanda nyingine? Katika kipindi cha miezi nane tangu ruhusa ya mikutano hiyo, iliyokuwa katika kibano kwa miaka saba, Chadema imezuru mara tatu katika kanda hiyo, huku ikirudia ziara zake zaidi ya mara moja katika baadhi ya Mikoa ya ukanda huo. Mathalan, Mkoa wa Mwanza ndiyo uliofungua pazia la mikutano ya hadhara ya Chadema katika Viwanja vya Furahisha, Januari 21 mwaka huu na baadaye chama hicho kilirudi mkoani humo kwa oparesheni +255 Katiba Mpya Okoa Bandari zetu. Ilifanya hivyo pia, katika Mkoa wa Mara na hadi sasa tayari imeshatembelea Mikoa yote ya Kanda hiyo, ukilinganisha na kanda nyingine. Pamoja na ziara zake katika baadhi ya Kanda kama Magharibi na Kaskazini, lakini Kanda ya Ziwa ndiyo imeonekana kutembelewa zaidi ya nyingine. Kwa taarifa yako, kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, idadi ya watu katika Kanda ya Ziwa ni asilimia 30 ya Watanzania wote. Karibu robo tatu ya wananchi wa Tanzania wapo katika Mikoa ya Kanda hiyo. Kadhalika, Kanda hiyo yenye Mikoa sita ya Mwanza, Kagera, Shinyanga, Mara, Geita na Simiyu ndiyo inayotajwa kuwa na idadi kubwa ya wapiga kura. Msuli wa Chadema katika mikoa hiyo, unalenga kuimarisha nguvu yake kwa upande mmoja, lakini kurejesha ngome yake hiyo ya zamani kwa upande mwingine, kulingana na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema. Akizungumza na Mwananchi jana, Mrema alisema kihistoria, kanda hiyo ni ngome ya muda mrefu ya Chadema hadi mwaka 2015, akirejea uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2014, ambao chama hicho kilipata asilimia 48. “Ujio wetu tunafuata mipango kazi wetu wa ndani, lakini ukweli ni kwamba kanda ya ziwa ilikuwa ngome yetu hadi 2015 na takwimu ziko wazi kwamba uchaguzi wa 2014 tulipata asilimia 48,” alisema. Kwa sababu hizo, alieleza kinachofanyika ni kuendelea kuiimarisha Chadema zaidi katika eneo ambalo tayari ilishawahi kuwa imara. Hata hivyo, alisema kulingana na mpangokazi wa Chadema, baada ya Kanda ya Ziwa ziara zitafuata katika kanda ya Nyasa na kwamba tarehe ya ziara hiyo itatangazwa baadaye. Watu wa Kanda ya Ziwa Wingi wao katika mikutano si kigezo kwamba wanakupenda, watu wa kanda ya ziwa hupendelea kusikiliza mawazo mbalimbali hata kama hawakubaliani nawe, kama anavyoeleza kiongozi wa moja ya makabila ya watu wa Kanda hiyo, Tonisiza Antonia. Tonisiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Mchifu Tanzania, alisema kaliba ya watu wa kanda ya ziwa ni kupenda kuchanganya mawazo. “Wanaweza kukusikiliza lakini wakabaki kwenye kile wanachokipenda sio rahisi kushawishika, ingawa kwa sasa Kanda ya Ziwa ina watu mchanganyiko, wamechanganyika,” alisema. Kutokana na mchanganyiko huo, Tonisiza alisema wapo wanaoshawishika kwa hoja na sera nzuri, lakini wapo wanaobaki na mapenzi ya asili na hawabadiliki hata wangeambiwa kipi kipya. Ni eneo linaloamua uchaguzi Hoja ya siri ya chama hicho cha upinzani kuweka msuli wake, kanda ya ziwa imefafanuliwa na Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Mohammed Bakari aliyesema eneo hilo ndilo linaloamua uchaguzi. Hiyo inatokana na kile alichoeleza, ni kanda yenye Mikoa mingi, Kadhalika idadi kubwa ya watu ukilinganisha na nyingine nchini. Lakini, alisema mwelekeo wa siasa za kanda ya ziwa hautabiriki, hivyo kila chama kitatumia nguvu kiliyonayo kuhakikisha kinavuna wafuasi. “Kuna Kanda unaziona kabisa zina muelekeo fulani, kwa mfano ukanda wa Pwani na Kusini unashabihiana na chama tawala, lakini upinzani una nguvu zaidi Kaskazini na Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Ziwa ni kugawana,” alisema. Alisisitiza hoja yake akisema ni eneo linaloamua muelekeo wa kisiasa, kwa sababu kuna wingi wa Mikoa na watu. Hata hivyo, Profesa Bakari alisema tangu uchaguzi wa kwanza wa siasa za vyama vingi, kanda ya ziwa ndiyo iliyokuwa na kinyang’anyiro kigumu. “Ni eneo nyeti la kufanya siasa, hata tulipoingia kwenye siasa za vyama vingi, katika uchaguzi wa kwanza, kinyang’anyiro kikubwa kilikuwa katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa,” alisema. Historia ya Chadema Kanda ya Ziwa Katika uchaguzi wa mwaka 2010, Chadema ilishinda katika majimbo karibu 10 kati ya 43 ya Kanda hiyo na uchaguzi wa 2015, iliishia kutetea majimbo matano pekee. Hali ilikuwa ngumu zaidi katika uchaguzi wa mwaka 2020, kwa chama hicho kuambulia patupu, kikidai dosari za uchaguzi ndiyo sababu ya hali hiyo.
Vigogo kumiliki ardhi na watumishi wa ardhi kuwa na maslahi katika upimaji ni miongoni mwa mambo mag
Vigogo kumiliki ardhi na watumishi wa ardhi kuwa na maslahi katika upimaji ni miongoni mwa mambo magumu yatakayomkabili Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa. Kulingana na wabunge, ugumu wa wizara hiyo unakuja pale ambapo maeneo nyeti nchini yanamilikiwa na wale waliowaita vigogo, hivyo inahitaji moyo wa chuma kuwashughulikia. Kauli za wabunge kuhusu ugumu huo, zinakuja wiki moja tangu Mbunge huyo wa Ukonga aapishwe kushika wadhifa huo ambao awali, Dk Angeline Mabula ndiye aliyekuwa nao. Tangu alipoapishwa, Silaa ameonekana mara kadhaa kuzungumza na menejimenti ya wizara hiyo na msisitizo wake ni kuomba ushirikiano na kuwataka watumishi wake kumaliza migogoro ya ardhi ndani ya siku 100. Watumishi wazembe nao, ni miongoni mwa waliokuwemo katika ahadi za Silaa katika maneno yake ya awali baada ya kuukwaa wadhifa huo, akiahidi kula nao sahani moja. Pamoja na mwanzo wa ahadi na msisitizo wa utendaji, inamhitaji moyo wa chuma kwa kuwa nafasi yake hiyo ya kushughulika na ardhi si jambo lelemama, kama anavyoelezwa na wabunge wenzake. Akizungumzia ugumu huo, Mbunge wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara alisema inahitaji moyo kuwasaidia wananchi wa ngazi ya chini, ilhali maeneo nyeti ya ardhi yanamilikiwa na vigogo. Alisema maeneo yenye rutuba na ambayo yalikuwa yakikaliwa na kutumiwa na wananchi wa kawaida yalishachukuliwa na watu wenye fedha na madaraka. Ingawa si haramu vigogo kuyamiliki, Waitara alisema angalau wawe wameyapata kwa njia halali, kwani aghalabu huyachukua kwa nguvu ya fedha au madaraka. “Siyo kosa kabisa ila jambo la msingi ijulikane waliyapataje maeneo hayo maana kwa sehemu kubwa yalikuwa ni maeneo ya watu lakini kwa ubabe wa nguvu ya fedha au madaraka vilitumika kuwachukuliwa wananchi. “Masikini ni masikini na bila kuungana atabaki hivyo, ardhi yako unaimiliki kihalali lakini anapewa mtu mwingine na ghafla anajenga au kuiendeleza, ukienda unaambiwa naye ana hati mwisho wa siku unaishia kwenye mgogoro,” alisema. Ujasiri, kujiamini na kufanya kazi bila upendeleo, ndizo mbinu za ushindi zilizotajwa na Waitara katika kuiongoza wizara hiyo, akisisitiza kinyume na hivyo Silaa atakwama. “Wizara ya ardhi sio lelemama na wakati wote itaendelea kuwa ngumu kama Tanzania haitaweka mkakati wa kuipima ardhi yote,” alisema. Pamoja na kueleza imani yake kwa Silaa, lakini Waitara alionyesha wasiwasi wa utekelezwaji wa kauli ya kumaliza migogoro ya ardhi ya siku 100. “Namwamini Silaa tangu nasoma naye chuoni, lakini napinga kauli yake kuwa ndani ya siku 100 migogoro itakwisha, haitekelezeki, ajue mingi itakwisha kwa njia ya kisheria ikiwemo mahakamani na mingine lazima iwe na ushirikishwaji hivyo kutoa matamko hakuwezai kumaliza,” alisema. Tabia ya kukosekana uaminifu iliyoota mizizi kwa baadhi ya watendaji wa wizara hiyo, ni moja ya maeneo ambayo Silaa ametakiwa kuyaangalia kwa jicho la pekee, kulingana na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Fatma Taufiq. Kwa mujibu wa Fatma, tabia hizo ndiyo chanzo cha migogoro, huku akisisitiza umuhimu wa kuwepo upimaji shirikishi. Alisema kumekuwepo na tabia ya wapimaji kuhitaji asilimia kadhaa wanapofanya shughuli hiyo na hivyo Silaa anahitaji ujasiri kuyakomesha hayo. “Watu wanamiliki maeneo yao tangu enzi za mababu zao, unakuja kupima halafu mwananchi mzawa wa eneo hilo unampa asilimia 60 au 40 ya ardhi yote aliyokuwa anamiliki halafu tena analipia, huu mpango si mzuri, namuamini Silaa na tutampa ushirikiano,” alisema Fatma. Pamoja na ushauri huo, Fatma alimtaka Silaa kuanza na migogoro inayotatulika, mathalan umilikishwaji ardhi kwa mtu zaidi ya mmoja. Aanze upya Kumbe mpango wa kamati ya mawaziri nane, haukuwa mujarabu kulingana na mtazamo wa baadhi ya wanasiasa, wakimtaka Silaa aachane nao na akaanze upya, kama inavyofafanuliwa na mmoja wa wabunge wa Kanda ya Ziwa aliyeomba hifadhi ya jina lake. Kufeli kwa kamati ya mawaziri nane, alisema kumetokana na kufanya kazi bila kuwashirikisha wananchi, waliishia kukutana viongozi na walichokiamua hakikuungwa mkono. Mbali na ushauri kutoka kwa wabunge wenzake, Silaa alipata baraka za utendaji kutoka kwa mtangulizi wake, Dk Angeline aliyesema yupo tayari kumpa ushirikiano wa kila namna. Mwanzo na maelekezo Mwanzo wa uongozi wake katika wizara hiyo umekumbana na maelekezo kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu, Dk Dotto Biteko aliyemtaka kuhakikisha ardhi inapangwa, kupimwa na kumilikishwa kwa ufanisi ili kuondoa migogoro. Alitaka wizara hiyo isigeuke kuwa mtatuzi wa migogoro, badala yake isimamie jukumu lake ya msingi ambalo ni kupanga, kupima na kumilikisha ardhi ili kuondoa migogoro. “Kazi za Wizara hii ni tatu, kupanga, kupima na kumilikisha ardhi, sasa tujipime na tujitathmini kama katika sekta yetu ya ardhi tunazifanya kwa ukamilifu wake. “Lipo wimbi la kuweka tension ya wizara kutoka kwenye sheria yake au Ilani ya uchaguzi na kugeuka kuwa Wizara ya utatuzi wa migogoro, kuanzia sasa tuwafanye watanzania wazungumze mipango miji, maendeleo ya makazi na matumizi bora ya ardhi,” alisema Dk Biteko alipofungua kituo cha taifa cha ubunifu na mafunzo ya taarifa za kijiografia jijini Dodoma.
Upinzani dhidi ya elimu ya miaka mitatu ya Katiba kwa wananchi kabla ya mchakato wa mabadiliko yake
Upinzani dhidi ya elimu ya miaka mitatu ya Katiba kwa wananchi kabla ya mchakato wa mabadiliko yake unaendelea kushika kasi, baada ya wadau kuitaja hatua hiyo kama mbinu ya kuchelewesha. Kauli hiyo ya wadau inakoleza moto kwenye hoja za mawaziri wakuu wastaafu, akiwemo Joseph Warioba, Cleopa Msuya na Frederick Sumaye, ambao nao walionyesha kupinga hatia hiyo ya elimu. Mpango wa elimu ya miaka mitatu ya katiba kwa wananchi, ulitangazwa Agosti 28, mwaka huu na aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro aliyesema utafiti uliofanywa umebaini zaidi ya asilimia 50 ya wananchi hawaijui Katiba. Kwa sababu hiyo, Dk Ndumbaro ambaye sasa ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, alisema Serikali imeamua kuanza na mkakati wa elimu ya miaka mitatu kwa wananchi, jambo lililoibua upinzani. Katika hoja yake kupinga mkakati huo, Sumaye aliwahi kuiambia Mwananchi hata ingetolewa miaka 10 ya uelimishaji isingelitosha wananchi kuielewa Katiba, lakini alisisitiza haja ya elimu iambatane na mchakato wa mabadiliko. Warioba yeye aliibuka na hoja ya uelimishaji uliofanyika mwaka 2014 alipokuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba enzi za utawala wa Jakaya Kikwete, akisema hakuna sababu ya kurudia hilo. Lakini, Msuya alionyesha upinzani kwa hoja ya kutokuwepo sababu ya elimu ya miaka mitatu ya Katiba, badala yake yaangaliwe maeneo yenye mapungufu na maboresho yafanyike. Juzi, wakichangia mjadala wa Mwananchi X-Space unaoendeshwa na Mwananchi Communications Limited (MCL), ukiwa na mada inayosema, “Nini maoni yako kuhusu miaka mitatu ya elimu ya Katiba kwa wananchi?” Katika mjadala huo, Mhariri wa Siasa wa gazeti la Mwananchi, Saleh Mohamed alitaja yapatikane maridhiano ya kitaifa yatakayowezesha kutoka kwenye mkwamo uliopo. Katika hoja yake hiyo, Saleh alionyesha mashaka na mpango wa Serikali kutoa elimu ya miaka mitatu kwa wananchi, kuhusu Katiba iliyopo. “Hapa tulipo lazima tupate maridhiano ya kitaifa, tunatokaje hapa tulipo na hata huu mpango wa Serikali kutoa elimu kwa miaka mitatu unatia mashaka kidogo,” alisema. Mjadala wa Katiba unatokana na alichoeleza kuwa, wapo wanaodhani ikiboreshwa itarahisisha safari yao ya kuingia madarakani, huku wengine wakiamini kuboreshwa kwake kutawaondoa katika madaraka. “Tatizo liko kwenye ubinafsi, hatujaamua kuweka maslahi ya taifa mbele. Ili tutoke hapa lazima tuondoe ubinafsi, tuweke maslahi ya Taifa mbele,” alisema Saleh. Akichangia mjadala huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga alisema mchakato wa Katiba ndiyo elimu yenyewe na yeye binafsi aliijua vizuri Katiba wakati mchakato ulipoanza kwa kuwa vyuoni hawafundishwi kwa kina. “Kuna watoto walikuwa wadogo hawakuwepo wakati Katiba inaandikwa lakini mbona hatukupewa elimu. Ndiyo maana kuna vitabu vya historia, kuna maktaba. Tuna nyaraka nyingi za kurejea,” alisema Henga. Mkurugenzi huyo alisisitiza kwamba amejiuliza dhamira ya Serikali kutaka kutoa elimu hiyo nini lakini hajapata majibu. Huku akieleza Tume ya Jaji Joseph Warioba ilikuwa akitoa elimu wakati akichukua maoni ya Watanzania, kwa hiyo inawezekana mambo hayo yakaenda sambamba. Henga alibainisha kwamba katiba nzuri inajengwa kwa maridhiano ya kitaifa na maridhiano hayo yafanyike kwa mchakato wa haki. “Katiba nzuri ni katiba yenye maridhiano, hata mkichoka mnafanya mabadiliko ili mradi muwe mmeridhiana. Katiba siyo uzuri wa uandishi, ni hayo maridhiano, na maridhiano hayo yafuate mchakato wa haki,” Aliongeza kwamba Tume ya Thabiti Kombo iliyoandika Katiba ya CCM, ndiyo hiyo iliandika pia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 1977, hivyo hakukuwa na uwakilishi wa wananchi katika zama ambazo chama kilikuwa kimeshika hatamu. Mjumbe wa kamati kuu ya ACT Wazalendo, Ismail Jussa alihoji namna elimu ya Katiba itakavyotolewa na lengo ni kufikia Watanzania wangapi ili kuwa na sifa ya kusema sasa wananchi wanaijua Katiba. “Ukisema ukatoe elimu kwa miaka mitatu, ni kiwango kipi unachotaka ufikie? Hata wanasheria, siyo wote wanajua sheria zote, unakuta huyu amejikita kwenye sheria za jinai, huyu amejikita kwenye sheria za biashara, huyu amejikita kwenye sheria za Katiba na utawala. “Hata tukifanya utafiti kwa hao wanaoitwa watunga sheria, hebu wafanyiwe utafiti kidogo wapimwe uelewa wao. Lazima tutapata ambao hawaijui Katiba na wapo wanaoijua,” alisema Jussa. Kada huyo wa ACT Wazalendo kutoka Zanzibar alibainisha kwamba hata nchi zenye demokrasia iliyoendelea kama Marekani, huwezi kukuta hata asilimia 30 ya Wamarekani wanaijua Katiba yao. “Siyo kila mtu anajishughulisha kutaka kujua Katiba yote, anataka kujua masuala machache yanayomuhusu. Kwa hiyo suala la elimu ya katiba ni kupoteza muda, ni kujaribu kuahirisha jambo hili,” alisema Jussa. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Faraja Kristomus aligusia Katiba ya sasa imempa mamlaka makubwa Rais kiasi kwamba ana nguvu kuliko mihimili mingine ya Serikali. “Mimi nadhani tunahitaji Katiba ambayo italiwezesha Bunge kusimama lenyewe, itakayowezesha Mahakama kusimama yenyewe na waweze kumkosoa Rais pale anapokosea. “Hii inafanya nchi yetu kuwa na mhimili mmoja tu wa Rais na siyo mihimili mitatu kama inavyoelezwa,” alisema Dk Kristomus. Mdau wa Katiba mpya, Eyala Murori alipendekeza kuundwa kwa jopo la wataalamu wa sheria nchini ili waandike Katiba mpya itakayotumika kwenye uchaguzi mkuu wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024. Aliosema kuielewa Katiba hakuhitaji kuwa na digrii, elimu ya kidato cha nne au darasa la saba. Huku akihoji kwamba elimu ya miaka mitatu ni kama digrii, sasa Serikali ina mpango wa kutoa digrii ya Katiba kwa wananchi? “Kama muda umebaki mchache, liundwe jopo la wataalamu wa sharia, likae chini, lipitie Katiba ya sasa, wachukue na ile ya Jaji Warioba, baada ya wiki tatu au siku 90, waje na Katiba Pendekezwa, twende kwenye kura ya maoni, twende kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa tukiwa na Katiba mpya.”alisema Alisema Serikali inapoendelea kuchelewesha mchakato wa katiba mpya, inachochea hasira za Watanzania, jambo ambalo linaweza kuhatarisha amani na usalama wa Taifa hili.
“Nilipofika nje, nilishangaa kuwaona niliowaacha ndani tayari wako nje,” ni maneno ya Kurwa Magwa, m
“Nilipofika nje, nilishangaa kuwaona niliowaacha ndani tayari wako nje,” ni maneno ya Kurwa Magwa, mhariri wa gazeti la Mwanaspoti akielezea saa tatu za mshikemshike wa tukio la ajali ya moto, lililotokea katika Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL). Magwa ni miongoni mwa wafanyakazi kadhaa walioshuhudia tukio hilo wakiwa kazini, lililotokea saa 1 usiku muda ambao aghalabu wengine huwa tayari wamesharudi nyumbani. Tukio hilo lililotokea Agosti 29, mwaka huu katika chumba cha kuhifadhia vifaa mbalimbali vya MCL, kulingana na tathmini iliyofanyika limesababisha harasa ya Sh940 milioni. Mbio za kutoka ndani ya ofisi kukimbilia kusikojulikana, sintofahamu ya kipi kinapaswa kuanza kuokolewa na mayowe ni miongoni mwa yaliyoshuhudiwa na kusikika wakati wa tukio hilo. Milio ya ving’ora kwa takriban dakika tano, haikutosha kuwastua baadhi ya wafanyakazi juu ya tukio hilo, wengi walidhani vinajaribiwa, lakini uliposhuhudiwa moshi kila mmoja aliusaka mlango. “Nikiwa ofisini kwangu niliona moshi mzito unapanda juu, nilishtuka na sikujua kitu cha kufanya, baadaye nilipata akili ya kushuka chini kumueleza msimamizi wa uchapaji kuwa kuna moto," anasimulia Aliamini Adam mkuu wa kitengo cha picha katika kiwanda cha uchapishaji magazeti. Wakati akisubiri kianze kipindi cha pili cha mchezo wa mpira wa miguu kati ya Klabu ya Yanga na JKT, aliokuwa anafuatilia kwenye runinga, anasema ndipo tukio hilo lilipotokea. Kabla ya mapumziko, anasema vilianza kusikika ving’ora vya tahadhari kwa dakika tano, lakini hawakuhofu wakidhani ni kawaida kwani vimekuwa vikijaribiwa au wakati mwingine vinapiga kelele kwa sababu ya vumbi. “Lakini nilipoona huu moshi nikasema si wa kawaida, ndipo nilipoamua kushuka chini kuona ni nini kinaendelea nikiwa kwenye ngazi nikaona moshi unatokea stoo ya kuhifadhia vifaa. "Na laiti ukuta wa hili jengo usingekuwa mgumu nafikiri mimi ningekuwa wa kwanza kufa na hakuna ambaye angejua kama nilikuwa ndani kutokana na moshi mzito uliokuwepo,” anaongeza Adam. Baada ya kutoa taarifa kwa msimamizi wa uchapaji, Adam anasema vijana waliokuwepo walishirikiana kuvunja mlango kwa kupokezana hadi walipofanikiwa. “Walijaribu kuvunja kufuri kwa kutumia nyundo na machuma huku wengine wakiwa wameshika mitungi ya kuzimia moto ili mlango utakapofunguka waanze kuzima moto,” anasema. Wakati hayo yanaendelea, tayari taarifa za tukio hili zilishasambazwa katika makundi ya mtandao wa WhatsApp ya wafanyakazi wa MCL na juhudi za kuusaka msaada wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na kampuni binafsi zilianza. Licha ya gari la zimamoto la kampuni ya SGA kufika eneo la tukio saa 2:07 usiku, ilikuwa vigumu kuingia ndani kwa kuwa, askari wake hawakuwa na vifaa vya kuzuia moshi. Dakika tano baadaye gari la Jeshi la zimamoto lilifika katika eneo hilo na juhudi za kuzima zilianza kwa kushirikiana na wafanyakazi. Hali ilivyokuwa Ni tamu kusimuliwa, lakini chungu ikikutokea, ndivyo unavyoweza kusema kuakisi hali ya baadhi ya wafanyakazi waliokuwepo katika eneo la tukio hasa wale waliokuwa na magari mawili katika eneo la maegesho. “Nilipotoka nilimpa Rama funguo anisaidie kutoa gari moja, sasa sijui ilikuwa ni kuchanganyikiwa badala ya kwenda mbele akawa anarudi nyuma, ikabidi nimtoe nitafute mtu mwingine anayeweza kunisaidia,” anasema Joseph Damas, mhariri mtendaji wa gazeti la Mwananchi. Katika siku hiyo, hakuna aliyejali hadhi ya mavazi aliyovaa, hata wenye tai walitoka nduki mithiri ya wanariadha na balaa zaidi lilishuhudiwa kwa wale wenye vitambi. “Mimi niliposikia kengele nilidhani kikao cha wahariri, kumbe moto, muda huo nilikuwa nawaza mpira, tulikuwa tunasubiri kipindi cha pili cha mechi ya Yanga na JKT,” anasema Charles Abel mwandishi wa gazeti la Mwananchi na Mwanaspoti. Kwa Salome Gregory anayeandikia gazeti la The Citizen, hakufikiria milango ya kawaida kujinusuru, tukio hilo lilimkumbusha kuisaka milango ya dharura ambayo hata hivyo alishindwa kuitumia kwa kutojua zilipo funguo. “Naujua mlango mmoja wa dharula lakini niliwaza funguo yake inakaa wapi ili nitoke nikakosa jibu,” anasema. Ilikuwa vigumu kuamini taarifa za simu, baada ya kupigiwa, Ibrahim Yamola, ambaye ni mhariri msaidizi wa gazeti la Mwananchi, alifunga safari hadi ofisini ajionee mwenyewe na alipofika aligonga kengere ya hatari. “Niliwaambia watu wa chumba cha habari kuna moto nje hivyo tunapaswa wote tutoke,” anasema Yamola. Taarifa zilivyofika Kwa kuwa ni wafanyakazi wachache ndiyo waliokuwepo ofisini, baada ya taarifa hizo walilazimika kurudi kama anavyoeleza Meneja wa Kitengo cha uzalishaji, Verspery. “Nikiwa njiani nilidhani ni stoo ndogo nikawa nawapigia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wakate umeme lakini sikufanikiwa. Nilipofika nilijaribu kutaka kuzima umeme, lakini moshi ulishatanda na hivyo nilishindwa,” anasema. Wingi wa moshi, anasema ulisababisha hata askari wa zimamoto kumwaga maji katika eneo lisilo sahihi. Kuungua kwa chumba hicho, kumeacha simanzi zaidi kwa Mtunza stoo wa MCL, Stella Joseph anayesema anajiona hana kazi ya kufanya kwa sasa kwa kuwa ofisi yake imeungua. “Sikuwa naelewa kitu cha kufanya, kuna vitu vingi sana vya thamani vya kiwandani vyote vimeungua na sielewi chanzo chake. Siku moja kabla ya moto kulikuwa na mzigo mpya umeingia na haukuwa umefunguliwa kwa muda huo ukitarajiwa kuanza kutumika siku inayofuata kabla ya tukio kutokea,” anasema Stella. Moto ulivyoathiri shughuli Vichwa vya wahariri watendaji wa magazeti ya Mwananchi, Mwanaspoti na The Citizen siku hiyo, viliwaza namna watakavyofikisha bidhaa sokoni katika mazingira hayo. Hiyo ilitokana na ukweli kwamba, moto ulitokea katika chumba kilichopo karibu na kiwanda cha uchapaji wa magazeti hayo wanayoyasimamia. Katika mazingira hayo, uamuzi wa haraka wa kuwasiliana na kampuni za nje za uchapishaji ikiwemo Jamana Printers zilifanyika na kufanikiwa. Pamoja na mafanikio hayo, kulikuwa na athari katika muda wa kufikisha bidhaa hiyo sokoni, kwani yalichapwa kwa kuchelewa kutokana na dharura hiyo. Kwa mujibu wa Damas, hadi moto unatokea tayari asilimia 95 ya gazeti lilishachapwa, zilibakia kurasa za michezo na ilisubiriwa habari kuhusu mechi ya Yanga na JKT. “Tunatakiwa tumalize gazeti saa 2:30 usiku lakini siku hiyo Saa 6 usiku ndiyo gazeti zilienda kuchapishwa The Guardian, gari zetu nyingi hazikuwa njiani kwa wakati huo zililazimika kusubiri, kuna baadhi ya Mikoa hatukwenda kabisa tulilazimika kupunguza oda na tuliangalia soko la mikoa ya jirani, pamoja na vituo vikuu mikoa ya mbali tuliamua kutokwenda,” anasema. Kulingana na Damas, magazeti yalikwenda katika Mikoa ya Morogoro, Iringa, Dodoma, Arusha na Mbeya, lakini baadhi ya maeneo likiwemo Jiji la Mwanza lilikosa kwa kuwa muda wa kusafirisha kwa ndege ulishapita. Lakini, uwezo wa kusoma mtandaoni kupitia EGazeti anasema uliendelea kuwepo na kesho yake uzalishaji uliendelea kama kawaida. Mbali na athari katika mauzi, Magwa anasema baadhi ya wafanyakazi walilazimika kurudi ofisini kumalizia kazi, baada ya moto kudhibitiwa. Hali hiyo, iliwaathiri hata wasanifu kurasa ambao ndiyo hufanya mchakato wa mwisho kabla ya gazeti kwenda mtamboni kama anavyosimulia, Himid Nyombwe anayefanya kazi hiyo. “Saa 9 alfajiri ndiyo niliingia nyumbani kwangu, hii ni baada ya kuhakikisha magazeti yote yamechapishwa huku wenzangu wakifika saa 10 alfajiri,” anasema. Mshutuko kila sehemu Mhariri Mtendaji Mkuu wa MC, Victor Mushi anasema ilimchukua muda kuelewa kuhusu tukio hilo, hata baada ya kuelezwa, lakini baadaye alielekeza gari lake litolewe nje kisha kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wote. Baada ya gari lake kuwa nje, anasema alihofu iwapo kwenye chumba cha habari kuna mfanyakazi yeyote aliyebaki. "Miongoni mwa mafunzo tuliyojifunza ni MCL inahitaji kuwa na njia iliyopangwa zaidi ya kushughulikia dharura hizi ili sote tujue inapotokea ni kitu gani kitakachotangulia kabla ya kufanya kitu chochote," anasema. Sebastia Koha Meneja wa Teknolojia ya Habari (Tehama), anasema mpango wa majanga umesaidia kubadilisha mfumo wa uchapaji kwa haraka ingawa sio kwa kiwango kilichozoeleka. "Tayari tulishaweka vitu vingi katika mipango ya majanga na ndiyo sababu tulipeleka kwa wachapaji wengine na tukafanikiwa kuchapa magazeti yetu,” anasema. Kuhusu tukio hilo, anasema alipopokea taarifa alidhani ni kiwanda chote kinaungua, hali iliyomsababishia mfadhaiko na hivyo kushindwa kuendesha gari. Kwa sasa, anasema wanajadiliana kuwa na utaratibu wa kuzima mitambo kisha kuchapa magazeti katika kampuni nyingine mara mbili kwa mwaka, ili kujijengea utayari wa majanga. “Hili ni eneo la kupata kipato chetu cha kila siku halafu unaona kunaungua inamaana hapo akili inayokuja kwa haraka inakuaje kuhusu kipato na ndiyo maana vijana walikuwa wanapambana kuzima moto,” anasema. Anasema hata vijana kukubali kuingia kwenye hatari yote ni kwa ajili ya kupambania riziki yao. Tukio hilo, lilimtoa chozi Thadeus Kisaka mbeba vifaa wa stoo za MCL akisema, "Watu wananiuliza kwanini ulilia siku ya tukio sababu kubwa niliwaza maisha yangu yatakuaje kwa kipindi hiki kuanza kutafuta kazi sehemu nyingine kwa haraka napata wapi na wakati huo nilitoka hospitali dada yangu kajifungua ndiyo sababu ya kulia na kupambana kuuzima moto." Lakini wengine, walikuwa mithiri ya waokozi katika tukio hilo, mathalan Esther Mvungi mhariri wa gazeti la Mwananchi, aliyeamua kumchukua mmoja wa wafanyakazi aliyekuwa mjamzito na kumrudisha nyumba ili kumuepusha na madhara ya moshi. "Kadiri muda ulivyokiwa unasonga ndivyo hali ya afya kwa baadhi ya watu ilikuwa mbaya hivyo niliamua kuondoka na mmoja wa wafanyakazi ambaye ni mjamzito na kumrudisha nyumbani kwake," anasema Mvungi. Hatua zinazochukuliwa Meneja Rasilimali watu na Utawala wa MCL, Paul Hamidu anasema wamepokea ushauri mbalimbali kutoka kwa wadau ikiwemo kuwa na visima vya kuzima moto. “Tumeambiwa kuna vifaa vya kisasa vyenye uwezo wa kudaka taarifa mapema tunatakiwa kuwa navyo kwa ajili ya kujikinga na majanga ya moto na hii itasaidia kwenye kupata taarifa,” anasema. Hata hivyo, anasema wafanyakazi mbalimbali waliokutwa na changamoto kutokana na ajali hiyo, wameshakwenda kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu kujua walivyoathirika. Mkurugenzi Mkurugenzi wa MCL, Bakari Machumu anasema hofu kubwa baada ya taarifa hiyo ilikuwa kwa wafanyakazi wake. Lakini, anasema alitamani kusikia tukio hilo ni dogo na kwamba limeshadhibitiwa, lakini haikuwa hivyo. Alipopewa taarifa kutoka kwa Hamidu, Machumu anaeleza alifika ofisini na kushuhudia moshi mzito. “Nilipofika mita 200 kabla ya MCL nilikutana na moshi, tunachoshukuru jengo la stoo ni imara sana, moto uliwaka zaidi ya saa nne, uharibifu mkubwa uliotokea kutoka mle lakini hautoka nje,” anasema. Anasema maboresho ya mtambo wa uchapaji yamefanyika usiku kucha kuhakikisha shughuli zinaendelea. “Tumefanya majaribio na tumethibitisha kwamba kazi inaweza kuendelea tuliwajulisha wateja wetu wa nje kuwa tupo sawa hivyo tunaweza kuendelea na kazi ya kuchapisha magazeti yao,” anasema. Hata hivyo, anasema mpango wa mafunzo ya kukabiliana na majanga kwa wafanyakazi wote yanatarajiwa kutolewa. Mwisho. Umoja wa BRICS unaundwa na nchi wanachama 11, badala ya tano zilizokuwa awali. Hatua hiyo, ni baada ya mataifa sita duniani kukubaliwa kuwa sehemu ya wanachama wapya wa umoja huo wa kibiashara duniani. Katika mkutano wa 15 wa nchi wanachama wa BRICS uliofanyika mjini Johannesburg, Afrika ya Kusini Agosti 24, mwaka huu. Wanachama hao wapya ni nchi za Argentina, Saud Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Misri, Iran na Ethiopia. Ongezeko la wanachama hao sita, wanafanya Umoja wa BRICS kuwa na idadi ya watu bilioni 3.3, sawa na asilimia 42 ya watu wote duniani, kadhalika asilimia 36 ya pato la dunia. Mbali na ongezeko la nchi wanachama, mkutano huo ulihitimishwa na matokeo chanya lukuki, ikiwemo kusitishwa kwa matumizi ya sarafu za ndani biashara kati ya wanachama wote na kwa mataifa yanayoendelea. Aidha, mkutano huo ulijadili kuhusu umuhimu na jukumu la benki mpya ya BRICS NDC kuunda sarafu ya pamoja ya BRICS pamoja na mfumo mpya wa kifedha wa benki hiyo. Kupanuka kwa BRICS na mipango yake ya kimkakati kumeibua matumaini ya kuimarika zaidi kwa ushirikiano wa kibiashara wenye faida sawa kwa pande zote na utakaokuza maendeleo ya Afrika. Matumaini haya yanatokana na ukweli kwamba nchi za BRICS zinapinga mawazo ya vita baridi na utawala wa upande mmoja. Kwa sababu hiyo, zimejitolea kukuza ushirikiano wa pande nyingi, kuheshimiana, kuaminiana na kushirikiana katika kuimarisha njia mbadala ya kimataifa ya kimaendeleo ambayo ni shirikishi. Tofauti na baadhi ya nchi zinazojaribu kuigawa dunia katika makundi na kupanua ushirikiano wao wa kijeshi ili kudumisha utawala wao, BRICS imejikita katika kudumisha amani ya dunia na kukuza maendeleo ya pamoja, yakiwemo ya Afrika Kwa kuzingatia kuongezeka kwa nguvu za kiuchumi na kisiasa za BRICS na kuongezeka kwa ushirikiano na nchi za Afrika, mataifa ya Afrika zinavutiwa zaidi na BRICS kwa sababu yanatoa fursa mpya za biashara, uwekezaji na uhamishaji wa teknolojia, itakayosaidia kukuza maendeleo na utangamano wa Afrika. Katika miaka ya hivi karibuni, nchi za BRICS, hasa China, zimepanua ushirikiano wao wa kiuchumi na Afrika. Kwa mfano, China ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Afrika na imefungua masoko muhimu zaidi kwa bidhaa za Afrika. Mathalan, mwaka 2022, asilimia 12.5 ya mauzo ya nje ya Afrika yalikwenda China, ikilinganishwa na asilimia 0.8 mwaka 2001. Kwa mujibu wa takwimu rasmi, thamani ya jumla ya biashara kati ya China na Afrika ilifikia kiwango cha juu cha dola bilioni 282 mwaka 2022, ikiwa ni asilimia 11 mwaka hadi mwaka. China pia imewekeza fedha nyingi katika miradi ya miundombinu na viwanda katika nchi za Afrika. Kama hiyo haitoshi, India nayo imeongeza biashara yake na uwekezaji barani Afrika, hasa katika nyanja za kilimo, huduma za afya, nishati mbadala, miundombinu, elimu na teknolojia ya habari na kuanzisha mfuko wa dola bilioni 10 kusaidia miradi ya maendeleo barani Afrika. Kulingana na takwimu ya Wizara ya Biashara na Viwanda ya India, katika mwaka wa fedha wa 2022/23, biashara kati ya India na Afrika ilikua kwa asilimia 9.26 hadi karibu dola bilioni 100, kutoka dola bilioni saba tu za mwaka 2001. Kwa sasa, BRICS ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara barani Afrika. Takwimu za utafiti wa kiuchumi wa mwaka 2022 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), zinaonyesha BRICS sasa ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Afrika huku biashara yao ikitarajiwa kuvuka dola bilioni 500 ifikapo mwaka 2030. Nchi za Afrika zimetambua kuwa kuzitegemea nchi za Magharibi kunazifanya kuwa hatarini, hasa pale maslahi yao yanapogongana. Ukweli kwamba zinalazimika kuuza mafuta na rasilimali zao nyingine kwa mataifa ya Magharibi kwa bei ya kupangiwa na kulazimika kufanya biashara kwa dola ya marekani na kutumia mfumo wake wa SWIFT wa kufanya miamala. Utaratibu huu unapingwa na nchi za Afrika kwa sababu nchi za Magharibi zimekuwa zikitumia dola, pamoja na taasisi kama vile IMF na Benki ya Dunia, kama chombo cha kiuchumi na kisiasa cha kudhibiti nchi hizo. Kutokana na mkakati mpya wa kifedha wa BRICS na ile hatua ya kuhimiza matumizi ya sarafu za ndani kufanya biashara, nchi za Afrika zinapaswa kutumia fursa hii kupigania uhuru kamili wa nchi zao na kuchukua hatua madhubuti ya kuondoa uchumi wao kutoka kwenye utegemezi wa mfumo wa dola na taasisi za Magharibi.
Mpango wa Serikali kutumia miaka mitatu kutoa elimu ya Katiba kwa wananchi, umeendelea kupata upinza
Mpango wa Serikali kutumia miaka mitatu kutoa elimu ya Katiba kwa wananchi, umeendelea kupata upinzani kutoka kwa Mawaziri Wakuu watatu wastaafu, baadhi wakihoji uelimishaji huo ni wa nini. Wakati wengine wakihoji hivyo, wapo wanaoshauri elimu inayotolewa isiathiri kuendelea kwa mchakato wa mabadiliko, wakisisitiza yote yafanyike pamoja. Licha ya maoni ya wanaopinga, wanasiasa wengine wakongwe wameonyesha kuunga mkono hatua hiyo ya elimu ya miaka mitatu kwa hoja kuwa, watafuata kile kinachoelezwa na Serikali. Mzizi wa upinzani huo ni kauli ya aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro Agosti 29, mwaka huu alipotangaza mkakati wa miaka mitatu ya uelimishaji wa wananchi kuhusu Katiba Mpya kabla ya kuuendea mchakato wenyewe wa mabadiliko. Kauli yake hiyo inatokana na kile alichofafanua, utafiti uliofanyika umebaini zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania hawaifahamu Katiba iliyopo na wengine hawakuwahi hata kuiona. Alipotafutwa kuzungumzia msimamo wa sasa wa Serikali baada ya maoni kinzani kutoka kwa wananchi wakiwemo viongozi wastaafu, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa alisema kwa sasa amejielekeza kwenye mkutano wa Jukwa la Mfumo wa Chakula (AGRF). “Naomba tuzungumzie kwamza AGRF kisha hayo mengine tuzungumzie baadaye kaka,” alijibu Msigwa. Mabadiliko ya Katiba ni mchakato unaostahili kuitwa mfupa mgumu nchini, kwani uliwahi kushika kasi wakati wa Serikali ya awamu ya nne, chini ya Rais Jakaya Kikwete, lakini mwaka 2014, ulikwama. Mkwamo huo, uliota mizizi hasa pale alipoingia Hayati John Magufuli (Rais wa awamu ya tano), aliyeweka wazi msimamo wake wa kutoendelea na mchakato huo. Matumaini ya kufufuka kwa mchakato wa Katiba Mpya, yalipatikana baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuingia madarakani na kuomba baraka za chama chake (CCM), kwa ajili ya kuukwamua. Maombi ya baraka hizo, yaliambatana na ahadi ya kuundwa kamati ya kushughulikia mchakato huo wa mabadiliko ya Katiba, jambo lililoongeza matumaini zaidi kwa wadau hasa wa siasa. “Swala katiba hakuna anayekataa hata chama changu hakuna anayekataa, na muda si mrefu tutatangaza kamati ambayo itashughulikia jambo hilo,” alisema Rais Samia Machi 8, mwaka huu alipohutubia Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani liliondaliwa na Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha). Pamoja na ahadi hizo, utekelezwaji wa michakato kuelekea mabadiliko hayo ndicho kitendawili kisichoteguka hadi sasa, huku kauli mbalimbali za Serikali zikiashiria haja ya kuwepo subira ya muda mrefu kabla ya kuifikia hatua hiyo na kauli ya Dk Ndumbaro ni kielelezo cha hilo. Akizungumza katika mahojiano na Kituo cha Runinga cha ITV, Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya alisema hakupaswi kutengwa muda wa miaka mitatu kuelimisha watu. Badala yake, alieleza kunapaswa kuangaliwa nini kinapungua katika Katiba ya sasa na kinarekebishwaje. "Tuone jinsi ya kushauriana na kufikia muafaka tuujumuishe katika marekebisho ya hiyo Katiba Mpya iliyopo tuendelee na kazi na watu waendelee na shughuli. “Kwa mfano unakuja kule kijijini kwangu kunielimisha kuhusu Katiba unamuelimisha nini kwa sababu hakuna Katiba standard duniani kote, kila nchi inatunga Katiba kulingana na mazingira na historia yake," alisema. Kwa mujibu wa Msuya, tume mbalimbali ziliwahi kuundwa hata wakati wa Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete akisema fedha nyingi zilitumika. Lakini, mtazamo wa Msuya ni tofauti na ile inayolenga kutungwa kwa Katiba nzima, akisema kinachohitajika ni kurekebisha mapungufu yaliyopo katika hii ya sasa. "Yafanyike marekebisho kulingana na nini kimeonekana kimepungua na kinaathiri uhuru na matumizi ya uhuru wa watu katika utendaji wa kazi," alisema. Alisisitiza tatizo sio elimu, bali kunahitajika kufanywa maboresho katika Katiba iliyopo kwa kuondoa maeneo yanayokera watu. Mtazamo wa Msuya, unafanana na wa Waziri Mkuu mstaafu wa Serikali ya awamu ya tatu, Frederick Sumaye aliyesema hata ingetolewa miaka 10 isingetosha wananchi kuielewa Katiba. Kinachopaswa kufanywa kwa mujibu wa Sumaye, wakati elimu inaendelea kutolewa, michakato mingine ya kufanikisha mabadiliko ya Katiba iendelee kufanyika. “Kuelimisha watu ni sawa lakini eti katika miaka mitatu kwamba watu watakuwa wamejua Katiba sio sahihi. Wakati tunaendelea na kuelimisha na michakato mingine ya Katiba ingeweza kuendelea,” alisema. Aliijenga hoja yake hiyo na kile alichofafanua, ingawa Katiba ni mali ya wananchi, wapo wanaopaswa kuijua kwa kina kwa niaba yao. “Wapo waliosoma na wapo katika vyombo vya sheria, lakini hawaijui Katiba ili wasome wanarejea kwenye vifungu mbalimbali,” alisema Sumaye. Hata hivyo, Sumaye alisema uelimishaji lisiwe jambo lenye ukomo liendelee kufanywa wakati wote. Pamoja na mtazamo wake huo, mwanasiasa huyo aliweka wazi haamini kwamba Katiba Mpya ndiyo utakaokua muarobaini wa shida za watu. “Kuna mambo mengi yanahitajika ili Katiba ifanye kazi sawa sawa,” alieleza kwa ufupi. Hoja kama hiyo, imetolewa pia na Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba aliyesema tayari wananchi wana elimu ya kutosha kuhusu Katiba Mpya na kinachopaswa ni kwenda kwenye mchakato wa kura za maoni. Kinachohitajika sasa, alisema ni utashi wa kisiasa kuliendea jambo hilo, au Serikali ieleze wazi kuwa Katiba mpya sio jambo la sasa hivi. “Tunachohitaji sasa ni utashi wa kisiasa, vyombo vya habari vinazungumza sana kuhusu Katiba Mpya, ndivyo vinavyofikisha ujumbe kwa Watanzania sambamba na vyama vya siasa. Wananchi wamepata elimu ya kutosha kuhusu Katiba Mpya,” alisema Warioba. Alieleza alipokuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba, walitoa elimu kwa wananchi hadi vijijini kwa kusambaza nakala za katiba ya Tanzania na Zanzibar na zote. Hatua hiyo ya Serikali, ilimuweka Joseph Butiku, katika mazingira magumu ya kutoa maoni akisema, “ilishashiriki kwenye kutengeneza maoni ya mabadiliko ya Katiba, ngoja wananchi waseme wanachoendelea kusema mimi sina maoni juu ya hilo.” Hali kama hiyo imetokea kwa, Waziri wa zamani katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Anna Abdallah aliyesema: “Ahhhhh… mimi sina maoni yoyote, kitakachoamuliwa na Serikali ndicho nitakachokisikiliza, mimi nitoe maoni ya nini tena,” alisema. Katika mazingira yaliyoshauriwa na Serikali, Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa alipendekeza njia aliyoiita sahihi ya upatikanaji wa Katiba, akitaka uandaliwe mjadala wa kitaifa utakaoshirikisha wananchi. “Mjadala wa kitaifa ndio mchakato wa kawaida katika taifa lolote katika upatikanaji wa Katiba Mpya na unasaidia kukubaliana na mambo ya msingi, sio sahihi kwa viongozi wachache kujifungia na kuamua au wanasiasa wengine wanavyoshauri,” alisema. Dk Slaa alisema Afrika ya Kusini ilianza na mjadala wa kitaifa, kisha ikatengeneza njia bora ya kufanikisha mchakato wa upatikanaji wa Katiba yao. “Kama tutapata haya (mjadala wa kitaifa) na watu kukubaliana, basi tutaona kuna nia njema na hatua ni utaratibu wa kufanya marekebisho ya mambo machache yatakayotoa ili mwaka 2024 tutafanye uchaguzi. “Sitaki kwenda bila umakini eti twende katika tume huru au kurekebisha sheria…Tukubaliane kwenye misingi, halafu wote kwa pamoja tuangalie utaratibu wa kupata vifungu vya Katiba vitakavyohakikisha kura za mwaka 2024/25 zitapigwa sawa na mtu atapata haki yake,” alisema Dk Slaa.
Hatua ya mamlaka ya uteuzi kutengua nafasi ya mteule muda mchache baada ya kumteuwa au kumbadilishia
Hatua ya mamlaka ya uteuzi kutengua nafasi ya mteule muda mchache baada ya kumteuwa au kumbadilishia wadhifa, imetajwa na wanazuoni, kuashiria changamoto katika mifumo ya uteuzi. Msingi wa hoja ya wanazuoni hao ni kilichofanyika Agosti 30, mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan alipomteuwa Profesa Kennedy Gaston kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Septemba 1, mwaka huu aliapishwa katika wadhifa huo. Lakini siku tatu baadaye, Septemba 3, mwaka huu uteuzi wake ulitenguliwa na aliteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hii si mara ya kwanza, ilitokea pia kwa Alexander Mnyeti aliyeteuliwa Septemba 30, mwaka huu, kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, lakini kabla ya kuapishwa alihamishiwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Hata Thobias Mwesiga alikumbana na hilo, Aprili 4, 2021, alipoteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kabla ya kuapishwa kesho yake alitenguliwa na James Mataragio aliteuliwa kuendelea na nafasi hiyo. Dk Raphael Chegeni naye, aliuonja wadhifa wa Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa siku tatu, kuanzia Julai 28, mwaka jana hadi Julai 31, mwaka huo alipotenguliwa na nafasi yake kuchukuliwa na Meja Jenerali Suleiman Mzee. Kama hiyo haitoshi, katikati ya uapisho, David Kafulila alihamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, badala ya Arusha na John Mongela akipelekwa mkoani humo, ikiwa ni siku mbili baada ya kuteuliwa. Hatua hiyo, imetajwa kuonyesha dosari katika mifumo ya uteuzi, kulingana na wanazuoni wa masuala ya sayansi ya siasa na utawala. Akizunguma na Mwananchi jana, Mhadhiri katika Idara ya Historia, Sayansi ya Siasa na Maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Clecensia Massawe alisema kuna haja ya kuangalia mifumo inayotumika kuwapata viongozi. “Mimi navyoona ni kama mifumo haijakaa sawa, kwa sababu hadi mtu ateuliwe kuna michakato imepitiwa, kwanini afikie hadi kuapishwa ndiyo aonekane hakuwa sahihi kwenye eneo hilo,” alisema. Alisisitiza akisema, “Kuna tatizo mahali. Haiwezekani watoto wako unataka mmoja umfanye kuwa Kiranja, unafika nyumbani unasema sijakuteuwa wewe nimpe mwingine.” Kutojitosheleza kwa taarifa anazopewa anayeteuwa ni sababu nyingine ya hali hiyo, kulingana na Mhadhiri wa Rasilimali watu na Utawala wa Chuo Kikuu cha Tumaini jijini Dar es Salaam (Tudarco), Dk Lazzaro Swai. Mhadhiri huyo alieleza kabla ya uteuzi, mamlaka yenye wajibu huo hupewa taarifa za mtu anayepaswa kuteuliwa kwenye nafasi fulani. Taarifa hizo, alisema ndizo zinazosababisha uamuzi wa nafasi ipi mteuliwa anastahili na wakati mwingine taarifa zinazopatikana huwa chache na nyinyine huja baadaye wakati uteuzi ulishafanyika. “Anapopewa taarifa za mtu husika wakati tayari ameshafanya maamuzi, hapo anaweza akapuuza lakini akiona zinamuweka kwenye nafasi nzuri zaidi anabadilisha uamuzi na kutengua uteuzi,” alisema. Lakini, alisema kwa sababu mamlaka ya uteuzi ipo mikononi mwa Rais na Katiba imempa jukumu la kuteuwa kwa kushauriwa au kutoshauriwa, mambo kama hayo ni kawaida kutokea. “Pengine ameshauriwa vibaya na akateuwa baadaye akipata taarifa anafanya uamuzi mbadala, lakini anaweza akateuwa bila kushauriwa, baadaye akishauriwa anafanya mabadiliko,” alisema. …kuhusu majaji Uteuzi wa Profesa Gaston, uliambatana na uteuzi wa Majaji 24 wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu nchini, akiwemo Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Aisha Sinde. Pamoja na kupongeza kuteuliwa kwa Aisha kuwa Jaji wa Mahakama Kuu nchini, Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Harold Sungusia alisema hatua hiyo inaondoa kigezo cha kiongozi huyo kuwawakilisha mawakili. “Moja kwa moja anapoteza vigezo vya kuendelea kusimama kama wakili anayewawakilisha mawakili wenzake. Ataendelea kuwa na uwakili wake lakini hatautumia, kwa sababu hatafutwa kwenye orodha ya mawakili wa Tanzania,” alisema. Lakini, alisema hauwezi kuwa Jaji wakati huo huo ukafanya kazi za uwakili, hapo ndipo kigezo cha kuwa kiongozi wa mawakili kinapoondoka. Hata hivyo, Sungusia alisema sheria na taratibu za TLS zipo wazi juu ya kujazwa kwa nafasi yake, akiyataja mambo mawili yanayoweza kufanyika. Jambo la kwanza, kulingana na Rais huyo wa TLS ni Baraza la Uongozi la chama hicho kumchagua mmoja wao mwenye sifa za vigezo vya kushika wadhifa huo na akawa Makamu wa Rais. “Kigezo cha kuwa Makamu wa Rais kwa mujibu wa sheria zetu ni kuwa na uzoefu wa kufanya shughuli za uwakili kwa miaka 10, hivyo kama yupo mwenye kigezo hicho ndani ya baraza la uongozi la TLS atachaguliwa na kushika wadhifa huo,” alisema. Lakini, kama atakosekana ndani ya baraza, Sungusia alisema kamati ya uchaguzi itaangalia miongoni mwa mawakili wenye sifa na vigezo na kuanza mchakato wa kumpata kujaza nafasi hiyo. “Inawezekana kabisa mtu akawa ndani ya baraza la uongozi lakini asiwe na sifa ya kuwa Makamu wa Rais, kwa sababu kigezo cha kuwa ndani ya baraza ni kufanya shughuli za uwakili kwa miaka saba, lakini kuwa Makamu ni kuwa wakili kwa miaka 10,” alisema. Mbali na hayo, Sungusia alipongeza uamuzi wa Rais Samia, kuteuwa mawakili wa kujitegemea, akisema alichokifanya kimethibitisha kuiishi falsafa yake ya R4. “Tulipokutana naye Ikulu tuliomuomba tujenge mahusiano bora kati ya mawakili wa kujitegemea na wa Serikali na tuliomba kwenye uteuzi wazingatie hilo,” alisema. Hiyo, alisema itaimarisha afya ya mahakama kwa kuwa na watu wenye mawazo mbadala. Alipotafutwa kuzungumzia uteuzi huo, Jaji Mteule Aisha Sinda alisema ni mapema mno hivyo, vugumu kueleza chochote. “Siwezi kuongea chochote kwa kweli, hapana… hapana…,” alijibu Makamu huyo wa Rais wa TLS. Mbali na Aisha wengine walioteuliwa ni Griffin Mwakapeje, Dk Dafina Ndumbaro, Emmanuel Kawishe, Abdallah Gonzi, Kamazima Idd, Frank Mirindo, Hadija Kinyaka, Hussein Mtebwa na Irene Musokwa. Wengine ni Ntuli Mwakahesya, Sarah Mwaipopo, Dk Angelo Rumisha, Said Ding’ohi, Ferdinand Kiwonde, Martha Mpaze, Anord Kirekiano, Sharmillah Sarwat, Wilbert Chuma na Dk Evaristo Longopa. Kwa upande wa majaji wa mahakama ya rufani walioteuliwa ni Jaji Abdul-Hakim Issa, Jaji Mustafa Ismail, Jaji Paul Ngwembe na Jaji Lameck Mlacha. Mchakato wa uteuzi wa majaji, huanzia kwa Jaji Kiongozi kwa kupeleka hoja ndani ya Tume ya Mahakama, kwa kuwa kiongozi huyo ndiye anayejua mahitaji ya watumishi hao. Katika maelezo yake kuhusu mchakato huo, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma aliwahi kusema baada ya hoja hiyo ya Jaji Kiongozi majina ya majaji wanaoteuliwa hupendekezwa kutoka sekta ya sheria, ikihusisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Taasisi za Umma. Kwa mujibu wa Profesa Juma, tume huwaandikia wadau kupendekeza majina ambayo baadaye huchambuliwa kwa kuzingatia vigezo, kisha kupelekwa katika ofisi ya Rais kwa uteuzi.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza uamuzi wake wa kuweka mkakati wa kuelekeza n
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza uamuzi wake wa kuweka mkakati wa kuelekeza nguvu zake vijijini kwa kuwa ndilo eneo lenye changamoto lukuki. Uamuzi huo wa Chadema unaenda sambamba na kile ilichokieleza, itaimarisha uongozi wa mabaraza yake yote kuanzia ngazi ya vitongoji. Hayo yameelezwa leo, Septemba 3, 2023 na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alipohutubia mkutano wa hadhara katika ziara ya Oparesheni +255 Katiba Mpya, Okoa Bandari Zetu. Uamuzi huo wa Chadema unatokana na kile kilichoelezwa na Mbowe, katika ziara yake na viongozi wa chama hicho, ameshuhudia changamoto nyingi vijijini. Alitolea mfano ziara yake katika vijiji vya mkoa huo, imemfanya kubaini tatizo la maji katika vijiji vyote vya Kanda ya Ziwa, uhalisia ambao haulingana na takwimu zinazotolewa na Serikali. Mbowe alisema Serikali imekuwa ikitoa takwimu za uongo kuhusu hali ya usambazaji wa huduma za maji katika maeneo hayo, ilhali uhalisia ni kinyume chake. “Watanzania wenzenu wa Mikoa hii yote ukilisikiliza Bunge, ukaisiliza Serikali inavyotoa takwimu za uongo kuhusu kumaliza tatizo la maji, nenda vijijini utaona hali halisi, utaona huruma,” alisema. Si maji pekee, alisema hata wakulima wa mazao mbalimbali ikiwemo Kahawa, pamba na tumbaku akisema ingawa watu wa mijini wanateseka, lakini shida zao ni robo ya zile za vijijini. “Sisi kama chama tuna kila sababu ya kupeleka moto wa kutosha vijijini, kwa sababu kama tunataka kubadilisha nchi hii, watu wanaoishi mijini ni asilimia 30 asilimia 70 wako vijijini wana hali mbaya kuliko maelezo,” alisema. Hali iko hivyo, ilhali wazalishaji wakubwa alisema wanatoka vijijini. “Hatuhitaji kumrejesha Yesu Kristo aje kusema CCM mmeshindwa kubadilisha uchumi wa nchi hii, leo hii Chadema ndicho chama pekee cha upinzani kimesimama na kinaweza kubadilisha maisha ya wananchi,” alisema. Lakini hilo, alisema litawezekana iwapo wananchi watakubaliana na chama hicho kupitisha azimio la Musoma litakaloamua kuachana na CCM. Alieleza chama hicho tawala kwa sasa kimebaki kuwa biashara ya watu kadhaa. Kiu ya chama hicho, alisema zaidi ya asilimia 70 ya viongozi wa Serikali za Mitaa katika uchaguzi ujao watokane na Chadema. Katika kufanikisha hilo, Mbowe alisema kinachotakiwa ni kuwepo uchaguzi huru na wa haki utakaoingia madarakani watu wenye hofu ya Mungu. Awali, akihutubia mikutano yake ya awali asubuhi, Mbowe hakuacha kuzungumzia mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uendelezaji wa Bandari nchini kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia kampuni ya DP World. Kuhusu hilo, alisema bandari ya Kibara mkoani humo ni miongoni mwa zile ambazo DP World itakabidhiwa. “Serikali ya CCM bila aibu inatwambia imeshindwa kuendesha bandari kwa hiyo njia pekee imeona ni kumkabidhi mwarabu bandari zetu,” alisema. Akikazia hoja ya viongozi kutokana na kutochaguliwa na wananchi, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu alisema hali hiyo inawakoseka wananchi kiongozi wa kumuomba msaada. “Katika hali hiyo kwanini kiongozi aliyepo madarakani awaheshimu wananchi wakati hawajamchagua,” alisema. Akihutubia mkutano wa hadhara mkoani Mara, Lissu alieleza pamoja na Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kueleza ‘ikiwezekana timiza wajibu wako’ lakini viongozi mbalimbali waliomfuatia walikiuka hilo. Aliithibitisha kauli yake hiyo na uongozi wa Hayati Benjamin Mkapa aliyeonyesha kushindwa na kuamua kubinafsisha mashirika ya umma. “Na kwenye hilo aliwahi kuandika kwenye kitabu chake kwamba kati ya vitu anavyojutia ni kubinafsisha mashirika ya umma na iwapo angepata nafasi ya kuwa Rais tena angelirekebisha hilo,” alisema. Jambo kama hilo, alisema limefanywa na Jakaya Kikwete kwa kuwapa wawekezaji kutoka nje ya nchi maeneo yote yenye gesi asilia baharini, kadhalika yale ambayo yanatajwa kuwa na mafuta. “Kwa sababu Kikwete alisema hayo sisi hatuyawezi tuwape wanaoweza wawekezaji, mafuta hayapatikani lakini wanayatafuta nayo alisema hatuyawezi, kwa hiyo kuna nchi zimegawiwa mapande mapande zinatafuta zikiyapata sio yetu,” alisema. Baadaye, alisema aliingia Hayati John Magufuli ambaye hakuwahi kuwapenda wageni, lakini alifanya kila kitu akinadi kuwa ni kwa fedha za Serikali ilhali alikopa kutoka nje ya nchi. “Ametuachia mzigo mkubwa wa madeni lakini hakuwahi kusema sisi hatuwezi,” alisema. Baada ya Hayati Magufuli, Lissu alisema amekuja Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ndani ya mwaka mmoja tangu kifo cha mtangulizi wake, akaenda uarabuni na ndiko lilikozaliwa suala la mkataba wa bandari. Katika hali isiyozoeleka, Lissu alimpongeza Hayati Magufuli kwa uamuzi wake wa kupinga kuwapa mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kwa Wachina. “Haukupita mwaka mmoja, aliyekuwa Makamu wake wa Rais amegawa bandari zote kwa muda usiokuwa na ukomo kwa wageni. Magufuli alisema ni kichaa ukigawa bandari moja kwa miaka 99 ni kichaa cha aina gani kinakuhusu ukigawa bandari zote bila ukomo,” alisema. Akiwa katika Jimbo la Mwibara mkoani mkoani Mara, Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Catherine Ruge alieleza kushangazwa na wakazi wa Mwibara kulalamikia changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji. Aliisisitiza hoja yake hiyo akiteleza ni miaka zaidi ya 60 tangu Tanganyika ipate uhuru, inawezekanaje kuwepo changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji. “Serikali ya CCM kwa miaka 62 ya uhuru imefali kutatua matatizo ya msingi ya wananchi, likiwemo hitaji la maji, kama wameshindwa maji wataweza kitu gani, tuwape miaka mingapi watatue keri ya maji,” alisema. Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, John Heche alisema Tanzania inahitaji ukombozi wa kiuchumi kwani inaagiza bidhaa nyingi za chakula kutoka nje ya nchi, ilhali kuna ardhi kubwa na nzuri ya uzalishaji. “Tuna viongozi madarakani ambao fikra zao zimefika mwisho, ni kikundi cha wanyang’anyi kinachoendelea kubaki madarakani kwa kutumia nguvu ya Polisi,” alisema. Iwapo viongozi wao wa CCM wakiendelea kuachwa wabaki madarakani, alisema itakuwa hatari na kwamba kunahitajika kufanyika mabadiliko.
Hatma ya nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Vijijini, Hanafi Msabaha na Mkurugenzi wa halmashauri hi
Hatma ya nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Vijijini, Hanafi Msabaha na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Tatu Issike imeamuliwa na wanachama 250 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kurudisha kadi za uanachama wa chama hicho. Uamuzi wa wanachama hao 250 kurudisha kadi za CCM, ulilenga kuishinikiza Serikali ikamilishe ujenzi wa mradi wa Shule ya Sekondari katika Kijiji cha Lyowa mkoani humo. Mzizi wa tatizo ni pale, Serikali wilayani humo ilipopeleka fedha za ujenzi wa shule ya sekondari ya Kata katika Kijiji cha Muungano badala ya Lyowa ambapo tayari wanakijiji walijitolea na kufanikiwa kujenga vyumba vitano vya madarasa, vyoo na ofisi za walimu kama walivyokuwa wameelekezwa. “Hizi kadi tunazirudisha kwa Mkuu wa Mkoa (Kanali Ahmed Abbas) hatuko tayari kuona pesa zinakuja za shule lakini zinapelekwa kijiji kingine wakati sisi tumejenga kwa nguvu hatujapewa hata Sh10 kwa nini tusisaidiwe,” alisema Ally Mtambulwa, mmoja wa wananchi. Kutokana na hilo, Rais Samia Suluhu Hassan alisema hatakuwa na imani na Mkuu wa Wilaya yeyote atakayesababisha kadi za chama hicho zirudishwe. Katika kuonyesha kuguswa na hilo, mkuu huyo wa nchi, alitangaza dhamira ya kuwafuta kazi jana viongozi hao Wilaya. Rais Samia alitangaza dhamira yake hiyo mkoani Pwani jana, alipohutubia hafla ya kufunga mafunzo ya uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa, iliyofanyika katika Taasisi ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani humo. Katika hotuba yake hiyo, mkuu huyo wa nchi alieleza uwepo wa baadhi ya Wakuu wa Wilaya wanaohongwa fedha kuhamisha miradi na kuamua itekelezwe katika maeneo mengine. “Mkuu wa Wilaya anahongwa, mradi anaacha kwenda unakotakiwa anapeleka usipotakiwa, kiasi kwamba wananchi wanafika kurudisha kadi za chama (CCM), sisi huku tuna haja kubwa mmetuacha fedha mmepeleka kule na kadi zenu hizo. “Sina imani na Mkuu wa Wilaya anayesababisha kadi zirudishwe, Mtwara, Mkuu wa Wilaya yako sijui Hanafi (Msabaha) namtimua leo siwezi kustahimili kadi za chama zinarudishwa, nini Mkuu wa Wilaya yupo DED yupo yeye na DED wake,” alisema. Mbaya zaidi, alisema baada ya kuulizwa wanajibu kwamba eneo ilipotakiwa kujengwa shule hiyo, kuna wananchi wa vyama vya upinzani zaidi. “Anaulizwa anasema unajua kule wengi wapinzani, so what (kwa hiyo) si Watanzania wale? Kwani wao sio watu, tena wamejenga maana kigezo ilikuwa wajenge atakayefika mbali ndiyo mradi upelekwe kwake,” alieleza. Hata hivyo, uamuzi wa wananchi hao uliambatana na kuifunga Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji, kwa kile walichoeleza ilishirikishwa na iliwataka kujenga madarasa matano, vyoo na ofisi ya walimu na wamefanya hivyo, lakini ilipopatikana fedha hawakupewa kukamilisha mradi. “Sisi hatuna maneno mengi watoto wetu hawataenda shule wala kazi hazitafanyika tunahitaji mpaka tujue sekondari yetu inakalimikaje na kwanini sekondari ya kata isijengwe hapa,” alisema mwanakijiji mwingine, Asha Issa Halikuishia hapo, sakata hilo lilisababisha hata kuondolewa madarakani kwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Hassan Mmunda. “Mimi nimetenguliwa nawaomba viongozi wa Serikali waje tukae tuongee naona maendeleo yamefanyika shule imejengwa lakini sasa shughuli za kiserikali zimesimama hii inaumiza hata watoto wetu wapo majumbani ofisi zimefungwa,” alisema. Baada ya uamuzi huo wa wananchi, Hanafi alisema Sh500 milioni zimepokelezwa kwa ajili ya ujenzi wa shule na kwamba zitatumika kujenga shule mpya katika Kata ya Muungano na ile ya Kijiji cha Lyowa itamaliziwa ili zifunguliwe pamoja. “Kila sehemu ilitaka shule ijengwe kwao, nikatumia busara ya kawaida baada ya kutembelea shule ya sekondari Lyowa ina eneo zuri kubwa limenyooka, lakini tayari kulikuwa na makubaliano yaliyotokana na vikao, vilivyopitisha ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kata ufanyike katika kijiji cha Muungano,” alisema. Msabaha ameiongoza Mtwara Vijijini kuanzia Januari 25, mwaka huu, kabla ya hapo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma. Lakini, Tatu amekuwa Mkurugenzi wa Mtwara Vijijini tangu Juni 6, mwaka huu alipoteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kushika wadhifa huo, kabla ya hapo alikuwa Ofisa Rasilimali Watu, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).
Ni kama wamewekwa kitanzini, ndivyo unavyoweza kuelezea kilichowakuta Wakuu wa Mikoa na Makatibu Taw
Ni kama wamewekwa kitanzini, ndivyo unavyoweza kuelezea kilichowakuta Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika hafla ya kufunga mafunzo ya uongozi, waliposhindwa kumuuliza lolote Rais Samia Suluhu Hassan. Hoja ya kuwa kitanzini inatokana na hatua ya Rais Samia kuwapa uhuru wa dakika tatu za kumuuliza chochote wasichokielewa kuhusu mafunzo hayo ya siku sita, lakini viongozi hao walishindwa kufanya hivyo. Kukosa kwao maswali, kulimfanya mkuu huyo wa nchi, awahoji iwapo wameelewa zaidi na kuweka msimamo kuwa yeyote atakayekwenda kinyume yatakuwa ni makusudi. Katika msisitizo wa kuwakemea watendaji wake, mkuu huyo wa nchi, alitangaza kuwafuta kazi, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Vijijini, Hanafi Msabaha na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Tatu Issike kwa kushindwa kusimamia vizuri wananchi. Rais Samia alitoa kauli hizo mkoani Pwani jana, alipohutubia hafla ya kufunga mafunzo hayo, yaliyofanyika katika Taasisi ya Uongozi ya Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani. Katika dakika tatu alizotoa kwa ajili ya kuulizwa maswali na walipokosekana wa kufanya hivyo, aliwachagua Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthon Mtaka na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga. Alipochaguliwa Mtaka alisema, “Mheshimiwa Rais kwanza shikamoo, kwa kweli mimi sina swali.” Maelezo hayo ya Mtaka yalijibiwa na Rais Samia kuwa, “umeyaelewa yote? Kwa hiyo ukienda ukitetereka unafanya makusudi.” Jambo kama hilo, lilipomgeukia Sendiga naye alisema, “sina swali zaidi ya shukrani, tunashukuru tumeongezewa ujuzi, maarifa na vitendea kazi kwenye vichwa kwa hiyo tutakwenda kuwajibika.” Baada ya kuuliza kwa msisitizo kuhusu yeyote mwenye swali na kukosekana alisema, “kwa hiyo mkienda mkifanya mtakuwa mnafanya makusudi si ndiyo? Lakini mmeshaelewa kila kitu. Haya.” ‘Msisubiri maelekezo’ Katika hotuba yake hiyo aliyosema hakuwa ameiandaa, mkuu huyo wa nchi, alisema ndani ya uongozi wake hatashusha maelekezo kwa viongozi kuhusu nini wanapaswa kufanya, badala yake anataka kuwaona wanakuwa na ndoto kulingana na mipango ya Serikali. “Usisubiri Rais aseme Mkuu wa Mkoa fanya hili huko, ile ilikuwa zamani, enzi za Mwanri (Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Tabora) mimi napenda kuona mtu anajituma, anajielewa anajua nini anafanya,” alisema. Lakini, aliwataka kusimamia maamuzi yao, huku akionya hilo lisiwafanye kutokubali ushauri wa wengine. “Naposema kusimama kwenye maamuzi yako sio muende huko kichwa ngumu mnachotaka ndo hicho hicho, hapana, unaangalia mazingira yaliyopo na unafanya kulingana na miongozo ya kisheria,” alisema. Katika hatua nyingine, Rais Samia alionyesha kukerwa na hatua ya Wakuu wa Mikoa kuficha siri za utendaji mbovu wa baadhi ya Wakuu wa Wilaya. Ingawa si mamlaka ya Mkuu wa Mkoa kumfuta kazi Mkuu wa Wilaya, Rais Samia alisema angalau hata wawatishie kuwasimamisha. “Kuna Mkuu wa Wilaya hasikii la mtu, hakai kituo cha kazi, ana miradi yake huko yeye kutwa anakuja anachuma anakwenda kujenga huko, kuna Mkuu wa Wilaya anatafuta ubunge kituoni hakai. “Anakaa siku mbili anakwenda huko anakotafuta ubunge, lakini Wakuu wa Mikoa mmenyamaza kimya mnafichiana huko, hamsemi. Mpaka apite Kassim Majaliwa (Waziri Mkuu) akirudi aah… mama pale Mkuu wa Wilaya hapana yule hatufai lakini Wakuu wa Mikoa kimya hamsemi na wale watu mmewaapisha wenyewe,” alisema. Awatimua DC, DED Mtwara Katika msisitizo wa usimamizi wa Wakuu wa Wilayam Rais Samia aliwafuta kazi Msabaha na Tatu, kwa uamuzi uliosababisha kero kwa wananchi hadi wakaamua kurudisha kadi 250 za CCM. “Mkuu wa Wilaya anahongwa, mradi anaacha kwenda unakotakiwa anapeleka usipotakiwa, kiasi kwamba wananchi wanafika kurudisha kadi za chama (CCM), sisi huku tuna haja kubwa mmetuacha fedha mmepeleka kule na kadi zenu hizo. “Sina imani na Mkuu wa Wilaya anayesababisha kadi zirudishwe, Mtwara, Mkuu wa Wilaya yako sijui Hanafi (Msabaha) namtimua leo siwezi kustahimili kadi za chama zinarudishwa, nini Mkuu wa Wilaya yupo DED yupo yeye na DED wake. “Anaulizwa anasema unajua kule wengi wapinzani, so what (kwa hiyo) si Watanzania wale? Kwani wao sio watu, tena wamejenga maana kigezo ilikuwa wajenge atakayefika mbali ndiyo mradi upelekwe kwake,” alieleza. Ashtukia mfumo wa upigaji fedha Alisema, “Nilikuwa Mbeya hivi karibuni kwenye Nanenane, nikakuta kadhia pale maofisa kabisa wa halmashauri wametengeneza mtandao wao, mbali na ule unaokusanya fedha za Serikali kiuhalisia kuna mwingine wa pembeni na umekusanya fedha nyingi sana. “Baada ya wao kufanikiwa wakawapa jirani zao , wakawapa jirani zao, nilikuwa nasubiri ripoti kutoka kwa Waziri (Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Tamisemi, lakini hajaleta bado na mimi nalijua na naendelea kufuatilia kwa njia zangu, sasa hiyo ripoti ije ikiwa diluted,” alisema. Alieleza hayo yanafanyika ilhali eneo hilo kuna Mkuu wa Wilaya, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkaguzi wa Ndani na Katibu Tawala wa Wilaya. “Unajiuliza hawa watu wote wanafanyakazi kule waliko au wanajifanyia kazi badala ya kufanyia watu, kwa sababu kama wote wapo kazini hili lingeonekana mapema, lakini kinachoonekana kuna mnyororo unaanza huko zinakatwa mapaka kila mtu anapata fungu lake,” alisema. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Angellah Kairuki alisema makundi yote ya watendaji yameshapatiwa mafunzo isipokuwa Wakurugenzi wa mamlaka za Serikali za Mitaa, ambao ya kwao yanatarajiwa kufanyika baada ya vikao vya bunge.
Huenda ikawa ngumu kushinda uchaguzi wa urais katika mazingira tata nchini, hili litatokea iwapo Ser
Huenda ikawa ngumu kushinda uchaguzi wa urais katika mazingira tata nchini, hili litatokea iwapo Serikali itatekeleza azimio la wadau wa siasa lililotaka uhuru wa kisheria wa kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais mahakamani. Uhuru huo wa kisheria ni moja kati ya maazimio 10 yaliyotolewa na wadau wa siasa katika mkutano wa kitaifa kuhusu hali ya demokrasia nchini, ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD). Kutungwa kwa sheria hiyo ni kilio cha muda mrefu cha wadau wa siasa, kinachokosoa Katiba ya Tanzania inayominya uhuru wa kuihoji Tume ya Taifa ya Uchaguzi (TEC), kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Rais. Nchi nyingi Afrika, kupitia katiba zao zimeruhusu matokeo ya urais kuhojiwa mahakamani, zikiwemo Uganda, Malawi, Afrika Kusini na Zimbabwe. Akitoa maazimio hayo wakati wa kuhitimisha mkutano huo jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa TCD, Profesa Ibrahim Lipumba alisema ni muhimu kuwepo uhuru wa kisheria kuruhuru matokeo urais kupingwa mahakamani. “Wadau wanataka kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi, mgombea binafsi ili kuwapa mwanya wasio na vyama, lakini uchaguzi wa Rais kuhojiwa mahakamani endapo kutakuwa na tatizo,” alisema. Pamoja na hilo, lingine lililoazimiwa ni ushindi wa rais uamuliwe kwa kupata kura zaidi ya 50, badala ya ilivyo sasa ambapo hata asilimia 15 zinampa nafasi hiyo ilimradi awe ameongoza. "Rais atangazwe ameshinda ikiwa amepata asilimia 50 jumlisha na moja ndiyo kiwe kigezo cha ushindi wake, hivi sasa hata ukiwa na asilimoa 15 ilimradi unaongoza utakuwa Rais," alisema. Alisema azimio lingine ni muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba kuwasilishwa bungeni pamoja na muswada wa mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa. Alieleza hatua hiyo ndiyo muafaka wa kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi kabla ya kufikia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025. Awali, kulikuwepo na hofu ya kufikia chaguzi hizo bila kuwa na tume huru ya uchaguzi, kwa kile wadau wa siasa walichoeleza, kumekuwepo na hali ya ucheleweshwaji wa mchakato wa mabadiliko ya Katiba. “Kwa sababu muda ni mfupi tukisema tuanze mabadiliko ya Katiba kisha sheria hatutaweza kuyakamilisha kwa muda muafaka," alisema. Azimio hilo kwa mujibu wa Lipumba, liliambatana na lile la kufanyika kwa mabadiliko madogo ya Katiba badala ya kuifumua yote. “Kwa sababu uchaguzi ni muhimu, washiriki wanaona uwezekano wa kukamilisha upatikanaji wa Katiba kabla ya chaguzi zijazo itakuwa ni kujidanganya. “Mkutano ulipendekeza kufanyika mabadiliko muhimu katika Katiba iliyopo sasa ili kupanua uwepo wa demokrasia na tume huru ya uchaguzi kuelekea uchaguzi ujao,” alisema. Hata hivyo, msingi wa azimio hilo ni hoja ya Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe aliyesema upo uwezekano wa kufanya mabadiliko ya sheria za uchaguzi kama hatua za awali, huku ule mchakato wa Katiba Mpya ukiendelea. Kinachohitajika, alisema ni utashi wa wadau kukubaliana kwamba hiyo ndiyo njia sahihi. "Ukiendelea mjadala wa nianze hiki, utafika uchaguzi bila hatua yoyote kufikiwa," alisema. Azimio lingine kwa mujibu wa Profesa Lipumba ni kuwepo uhuru wa kisheria utakaoruhusu matokeo ya uchaguzi wa Rais kupingwa mahakamani. Pamoja na hilo, lingine lililoazimiwa ni ushindi wa rais uamuliwe kwa kupata kura zaidi ya 50, badala ya ilivyo sasa ambapo hata asilimia 15 zinampa nafasi hiyo ilimradi awe ameongoza. "Rais atangazwe ameshinda ikiwa amepata asilimia 50 jumlisha na moja ndiyo kiwe kigezo cha ushindi wake, hivi sasa hata ukiwa na asilimoa 15 ilimradi unaongoza utakuwa Rais," alisema. Fomu zitolewe bure Katika mabadiliko ya sheria ya uchaguzi, Profesa Lipumba alisema wadau wameazimia kuondolewa kwa gharama za uchukuaji na urudishaji fomu ya uchaguzi katika nafasi mbalimbali ili kuongeza ushiriki wa wananchi kuwania uongozi. "Nakumbuka kwenye urais, inahitajika ukirudisha fomu upeleke na Sh1 milioni, sasa kuna watu wanataka kugombea urais na hawana hiyo fedha. "Unaweza kuwa huna Sh1 milioni lakini una mawazo mazuri ya kuwaletea Watanzania, kwa hiyo hiki kikwazo kiondolewe," alisema. Maazimio mengine ni mabadiliko ya sheria ya utumishi wa umma, ili kutoa mwanya kwa watumishi wa umma wanaoshindwa katika uchaguzi warejee kazini. Mzizi wa azimio hilo ni kauli ya Mratibu wa Kitaifa wa Ulingo, Dk Avemaria Semakafu aliyesema wanawake wanahofu kushiriki kugombea watapoteza nafasi zao katika utumishi wa umma. Akisoma azimio hilo Profesa Lipumba alisisitiza, “Hili linawakwaza wengi hasa wanawake ambao wengi ni watumishi wanaogopa kwenda kugombea wakikosa watakuwa wamepoteza ushindi na kazi," alisema. Utaratibu wa sasa, utumishi wa umma wa mgombea utakoma pale tu NEC itakapomtangaza kuwania nafasi ya uongozi. Maazimio mengine kwa mujibu wa Profesa Lipumba ni Serikali iwezeshe majadiliano baina ya vyama vya siasa, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na tume huru ya uchaguzi badala ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi). Lakini, yamo maazimio yanayovitaka vyama viwekewe sharti ya kisheria kwa vyama vya siasa kutoa fursa kwa wanawake na makundi maalum kushiriki katika ngazi za maamuzi. Profesa Lipumba alisema wadau hao waliazimia mabadiliko ya sheria ya Jeshi la Polisi ili iendane na mahitaji ya demokrasia Lingine ni kutumika kwa lugha nzuri na za staha katika katika majukwaa ya kisiasa. Serikali: ‘Tutatekeleza’ Akijibu maazimio hayo, Rais Dk Hussein Ali Mwinyi alisema Serikali itafanyia kazi. Si hayo tu, alisema haya mapendekezo mbalimbali kuhusu mabadiliko ya Katiba, pia yatafanyiwa kazi. Rais DK Hussein Ali Mwinyi alisema kuanzishwa kwa demomrasia ya vyama vingi kulisababisha mabadiliko ya sheria mbalimbali ikiwemo ya vyama vya siasa na ile ya tafa ya uchaguzi. Hata hivyo, alisema utaratibu wa kukaa pamoja kujadiliana masuala ya kitaifa ni dalili ya kukua kwa demokrasia na ukomavu wa kisiasa. “Kwa sasa kuna maendeleo kadhaa na Serikali inaendelea kufanyia kazi mapendekezo mbalimbali kuhakikisha demokrasia inaboreshwa,” alisema. Katika hatua nyingine, Dk Mwingi alizindua mradi wa kuwashirikisha vijana na wanawake katika siasa na uchaguzi. Mwakilishi wa ubalozi wa Uswisi, alisema kinachofanywa katika uongozi wa Rais Samua Suluhu Hassan, kinadhihirisha dhamira ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kidemokrasia. “Juhudi hizi ni ile falsafa ya R4, kuunda kikosi kazi, kufanya mikutano ya majadiliano kati ya wadau na TCD ni ishara ya dhamira njema ya uongozi wake kuifikia demokrasia,” alisema. Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Michael Battle aliwataka watanzania kuwa demokrasia inayoendana na mazingira yake, kwa ajili ya watu wake na itakayojengwa na Watanzania wenywe. “Watanzania lazima muamue demokrasia itakayoendana na mazingira yenu, kwa ajili ya watu wenu na itakayotekelezwa na ninyi wenyewe,” alisema.
Ni mjadala wa kupeana makavu, ndivyo unavyoweza kuuelezea mkutano wa wadau wa siasa kuhusu hali ya D
Ni mjadala wa kupeana makavu, ndivyo unavyoweza kuuelezea mkutano wa wadau wa siasa kuhusu hali ya Demokrasia nchini, uliohusisha minyukano ya hoja miongoni mwa viongozi wa kisiasa. Katika mkutano huo, uliohusisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa juu wa vyama vya siasa nchini, ilikuwa ni majibizano ya hoja. Baadhi ya hoja zilizoibuliwa zilielekezwa kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana aliyekuwepo kukiwakilisha chama hicho katika mkutano huo. Miongoni mwa hoja hizo ni CCM kuwa sababu ya kudorora kwa mchakato wa Katiba Mpya, lakini wapo waliotaka hakikisho la kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi kutoka kwa chama hicho tawala. Akijibu hoja hiyo iliyoibuliwa na karibu wadau wengi hasa kutoka vyama vya upinzani waliopata nafasi ya kuzungumza, Kinana alisema si ajabu kwa CCM kutajwa kuhusu hayo. Jawabu lake hilo linatokana na kile alichoeleza, ni CCM ndiyo inayoshika dola, ndiyo yenye Serikali na ndiyo cha kinachotawala hivyo hakuna namna ya kukwepa tuhuma hizo. Lakini, alitoa matumaini yake akieleza Tanzania itakwenda kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na Mkuu wa 2025 ikiwa na muafaka wa tume huru na haki. Majibu yake hayo, yametokana na kile alichokifafanua, kauli mbalimbali za Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Katiba Mpya, maridhiano na falsafa yake ya R4 ndizo zinazompa tumaini. "Sidhani hata kidogo baada ya Rais kutoa kauli nyingi sana juu ya dhamira yake ya Katiba Mpya, maridhiano na R4 zake, mimi naamini kwamba tutakwenda kwenye uchaguzi wa 2024 na 2025 tukiwa na muafaka wa jumla na maelewano yanayokidhi uchaguzi huru na wa haki," alisema. Aliunganisha majibu hayo na hoja ya Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliyesema ni vigumu kubadilisha sheria za uchaguzi bila kufanya mabadiliko ya sheria mama ambayo ni Katiba. Hoja ya Mnyika, ilisimamia msingi kwamba baadhi ya sheria za uchaguzi mabadiliko yake yanagusa vifungu vya Katiba, hivyo haitawezekana kuvibadili bila muswada bungeni wa sheria ya mabadiliko ya Katiba. Alisema muswada huo ndiyo utakaoruhusu kufutwa au kubadilishwa kwa vifungu hivyo katika Katiba. "Nasisitiza kwamba ni vigumu kujihusisha na mabadiliko ya sheria za uchaguzi bila kuanza na mabadiliko ya Katiba ama kwa ujumla wake au marekebisho ya baadhi ya vifungu (vya Katiba)," alisema. Kinana aliijibu hoja hiyo akieleza haamini kuwa mabadiliko ya sheria za uchaguzi yanahitaji kwanza, mabadiliko ya Katiba. "Kwa mfano tukisema tunataka kubadilisha sheria ya uchaguzi wakati imejieleza kwenye Katiba mnaweza kufanya mabadiliko kwenye sheria hiyo ikapigiwa kura kwenye Bunge na ikafutwa kwenye Katiba na ikabaki iliyopo," alisema. Hoja nyingine iliyoibuliwa dhidi ya chama chake ni kutoka kwa Msemaji wa CUF, Mhandisi Mohammed Ngulangwa, aliyesema chama hicho ndicho kilichosababisha mkwamo katika mchakato wa Katiba Mpya wa mwaka 2014. Hilo lilimuibua Mjumbe wa Kamati ya Utekeleza ya UWT, Hawa Ghasia aliyeeleza kushangazwa na kauli dhidi ya chama chake kuukwamisha mchakato huo. Alisema CCM ndiyo iliyoonyesha utashi wa kuridhia mchakato huo na kuunda tume ya mabadiliko ya Katiba, lakini hatimaye vyama vya upinzani vikasusia vikao wakati wa hitimisho. "Wenzetu mliamua kuacha kipindi ambacho tayari Dereva ameshapatikana na gari imeanza kutembea, leo hii kama CCM inataka huo uharaka ingeshafanya kwa sababu Una nguvu ya kuamua lakini hekima za Rais Samia ndizo zinazofanya mambo yaende hivi vizuri," alisema. Hoja ya Ghasia, ilimkosesha uvumilivu, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Juma Duni Haji aliyejibu kwa kueleza kuwa, sababu za upinzani kususia mchakato wa Katiba Mpya 2014, ni hatua ya CCM kwenda na Katiba iliyotoka mifukoni mwao. "Hatukukimbia mchakato tuliondoka baada ya kuona mnataka kutuletea Katiba yenu kutoka mifukoni sio Ile wananchi wanayoihitaji," alisema Duni. Minyukano haikuishia hapo, wapo walioibua hoja kuhusu usawa wa jinsia katika nipo la wazungumzaji wa kwanza ambao wote walikuwa wanaume. Hilo lilimuibua Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza aliyesema si bahati mbaya bali waliokuwepo ndiyo waliopendekezwa na vyama husika. "Tulileta mapendekezo kwa vyama vyenu, vikatuletea majina ya wanaume, nadhani ni changamoto ya usawa ndani ya vyama vyenu na sio sektretarieti," alisema. Lakini, mkutano huo pia haukuiacha Chadema, ambayo aghalabu hususia vikao vya Baraza la vyama vya siasa. Alipopewa nafasi ya kuzungumza, mwanasiasa mkongwe, John Cheyo alielekeza hoja yake kwa Mnyika akimwambia hakuna faida ya kususia mambo yenye maslahi ya kitaifa. Alitaka kuachwa utamaduni wa kususia kila kitu kwani hauipeleki nchi popote. "Nchi hii ni yetu wote si ya chama kimoja ni yetu wote, yakiharibika hapa hakuna pa kukimbilia," alisema. Mengine yaliyozungumzwa ni kuhusu uhuru wa maoni kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Chauma, Hashim Rungwe aliyesema uliopo una mipaka. "Binadamu kama hatakuwa na uhuru wa kuzungumza ujue ni matatizo katika jamii yenu ama nyumbani au katika taifa, lakini binadamu ameumbwa ili awe na fikra," alisema. Alieleza kila mtu anapaswa awe na uhuru wa kuzungumza isipokuwa asikiuke mipaka, mathalan kutoa lugha za matusi. Kwa mujibu wa Rungwe, wananchi wa Tanzania wamekuwa na uwoga wa kuzungumza wakidhani watafuatwa na vyombo vya dola, hivyo uhuru walionao umekuwa na mipaka. "Uhuru huu una mipaka yake, nimetoa kama ufupisho, lakini nafikiri Watanzania kwa ujumla wetu tuna haki ya kuzungumza hasa mambo yanayotukera, lazima uzungumze ili Serikali itusikie," alisema. Akijibu hilo, Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Joseph Selasini alisema uhuru unapaswa kuwa na mipaka hasa ya kuzingatia tunu za taifa. Pamoja na kuwepo uhuru, alisema hakupaswi kutolewa lugha chafu na matusi dhidi ya wanasiasa majukwaani. "Ikitokea mwanasiasa mmoja amekwambia mwingine kwamba Mwenyekiti wa Chama fulani ni mjinga unadhani anasababisha nini kwa wafuasi wa chama hicho, tuwe na lugha nzuri," alisema. Mkutano huo haukuishia kwenye majibizano ya hoja bali kulikuwepo maoni mengine. Mnyika alieleza kusikitishwa na ahadi za Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Katiba Mpya ambazo bado hazijatekelezwa. Lakini, alieleza masikitiko yake kwa ahadi iliyowahi kutolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Januari kuundwa kwa kamati za mchakato wa mabadiliko hayo lakini hadi sasa hazijaundwa. "Nisikitike pia, hivi karibuni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro ametoa kauli kwamba mchakato utaanza Septemba (mwaka huu) kwa kutoa elimu kwa wananchi, jambo ambalo lilishafanyika, njia hii si sahihi," alisema Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliyesema si tamanio lake kusikia mjadala unaojikita kwenye nchi ilipotoka na ilipo kwa kuwa hayo tayari yameshajadiliwa na yanajulikana. Hoja yake hiyo inatokana na alichoeleza, Katiba iliyopo ilitengenezwa kwa mfumo wa chama kimoja na ukurasa mpya wa kuandika Katiba Mpya ulianza mwaka 2012 lakini ulikwama 2014. Kwa sababu ya mkwamo huo na kuchelewa kukwamuliwa, Mnyika alisema ni muhimu kuandika Katiba Mpya sasa kama msingi wa mabadiliko ya sheria mbalimbali. Kwa kuwa maoni yameshatolewa, alisema ni muhimu kutafuta muafaka ili katika mkutano wa Bunge wa Septemba upelekwe bungeni muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba. Hata hivyo, alikiri kukua kwa Demokrasia nchini, ingawaje kulikuwepo hitilafu katika miaka michache iliyopita. Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, kulikuwepo na ongezeko kubwa la wawakilishi kutoka vyama vya upinzani na ingeendelea hivyo hata mwaka 2020 kama uchaguzi ungekuwa kama ilivyokuwa nyuma. Akiendelea kujenga hoja hiyo kwa kukiri mapungufu ya kisheria na usimamizi wake. Kuhusu Katiba Mpya, Kinana alisema pamoja na kuundwa tume mbalimbali na kupendekeza mabadiliko ya Katiba, lakini hayakuwahi kutekelezwa. Lakini, alisema katika Serikali ya awamu ya sita, angalau ameona dalili za kuwepo kwa mabadiliko ya Katiba. Kwa sasa, alisema kuna michakato ya namna ya kuipata Katiba, kadhalika mchakato mwingine unaendelea wa mabadiliko ya sheria za uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025. "Sheria hizi zitatazamwa upya ili kujibu matakwa ya demokrasia, nina hakika zikitazamwa na wote tukikubaliana na kupelekwa bungeni kwa namna tulivyokubaliana tutakuwa na uchaguzi huru na haki kuliko wakati wowote nchini Tanzania," alisema. "Lakini ukiniuliza je, demokrasia imekuwepo naam imekuwepo, je, kuna kasoro naam kasoro zipo ndiyo maana tunakutana humu ndani na tunakutana kupitia baraza la vyama vya siasa," alisema. Katika mjadala huo, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Juma Duni Haji alisema iwapo ataulizwa kuwa Tanzania ina Demokrasia au laa, atajibu iliyopo ni ndogo mno. "Tatizo tulilonalo ni kwamba demokrasia yetu imemilikiwa na Dola, tunaitazama CCM lakini hata yenyewe ingekuwa kama sisi ingelalanika," alisema. Alieleza vigezo vya Demokrasia ni watu kuwa huru, kuwa na Serikali iliyochaguliwa na watu kwa ajili ya watu na kuwepo vyombo vinavyolinda uhuru wa watu. "Hatujawa huru kuichagua Serikali tunayoitaka tukiwa huru, bahati mbaya sheria tumefungia wenyewe na Katiba tumetunga wenyewe lakini hatuzifuati," alisema. Alieleza kama Tanzania ipo tayari kuwa na demokrasia sheria zinazotungwa kuendesha uchaguzi alisema zinapaswa kufuatwa. "Hivi sasa bado sheria zetu, angalau mwaka huu zimalizike ili angalau itakapotoka uchaguzi wa Serikali za Mitaa tuwe na uchaguzi huru," alieleza. Hata hivyo, alisema tatizo la Tanzania ni kukosekana utashi wa kisiasa kwani makongamano lukuki yanafanyika bila utekelezwaji. "CCM tangu mwanzo hawakuwa wanataka vyama vingi na muda wote wanasimama kuhakikisha CCM inabaki madarakani wengine wanashindwa," alieleza. Alieleza kama taratibu zitafuatwa inawezekana kwa wawakilishi wa vyama vyote vya siasa nchini wawepo bungeni. Alieleza ingawa kutafanyika mabadiliko ya sheria lukuki, lakini hazitafaa kama hakutakuwa na utashi wa kufuatwa na kutekelezwa. "Unaweza kusema ibadilishwe yote, Bunge ni la CCM. Tukisema tusubiri mabadiliko ya Katiba ndiyo sheria za uchaguzi wakikataa tutashindwa," alisema. Kasoro katika tume Akichangia mjadala huo, Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Joseph Selasini alieleza kwa mfumo wa tume ya sasa, uchaguzi unasimamiwa na watu ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). "Tumekuwa na chaguzi lakini zimekuwa kama kiini macho kuonyesha tuna Demokrasia, lakini hazibebi utashi wa wananchi," alisema. Alieleza demokrasia imekuwa ikiingiliwa kwani wanaoshiriki uchaguzi wanajikuta kwenye mateso ya vipigo kutoka katika vyombo vya dola. "Hatuwezi tukaingia kwenye uchaguzi, chama fulani kina mabilioni ya fedha, kingine kina mamilioni ya fedha alafu kuna ambacho hakuna kitu kabisa," alisema. Alieleza ni vigumu kueleza kuhusu demokrasia ilhali vipo baadhi ya vyama visivyo na uwezo wa kufanya safari hata ya kilomita chache za kwenda kuelimisha jamii kuhusu demokrasia. "Watu wengi wana uwezo wa uongozi, lakini wanashindwa kuingia kwa sababu hawamudu gharama za kutafuta uongozi, tulifanya hivi tutaendelea kuwa na viongozi matajiri na wale wengine watabaki kama walivyo," alieleza. Akijibu kuhusu maana ya tume huru Selasini alisema ni mlolongo mzima wa tume husika kuanzia juu hadi chini. Alichopendekeza ni kuwepo chombo huru kitakachopendekeza kwa njia ya mahojiano watu ambao Rais atawateuwa kuingiza tume. Baada ya kuteuliwa, alieleza wao ndiyo wanapaswa kuandika kwamba nani anataka awe msimamizi wa uchaguzi eneo fulani na waajiriwe kuifanya kazi hiyo. "Tunapozungunza uchaguzi mkuu mwanzo wake ni uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hausimamiwi na sheria za uchaguzi bali unasimaniwa na Tamisemi," alisema.
Ni matumaini, ndivyo unavyoweza kuielezea kauli ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), A
Ni matumaini, ndivyo unavyoweza kuielezea kauli ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana akieleza Tanzania itakwenda kwenye uchaguzi wa 2024 na 2025 ikiwa na muafaka wa tume huru na haki. Kauli ya Kinana, inasadifu matarajio ya wanasiasa wengi ambao aghalabu wamekuwa wakidai tume huru ya uchaguzi kama karata yao ya ushindi katika chaguzi mbalimbali. Malalamiko mengi kuhusu tume ni kile kinachoelezwa, sheria zinazoisimamia zinawapa mamlaka watendaji wa Serikali (Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuwa wasimamizi wa uchaguzi. Kinana alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, alipojibu maswali ya wajumbe katika mjadala wa hali ya Demokrasia nchini, ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD). Imani yake hiyo, inatokana na maelezo kwamba, kumekuwa na kauli nyingi za Rais Samia Suluhu Hasaan kuhusu dhamira ya Katiba Mpya, maridhiano na R4 zake. "Sidhani hata kidogo baada ya Rais kutoa kauli nyingi sana juu ya dhamira yake ya Katiba Mpya, maridhiano na R4 zake, mimi naamini kwamba tutakwenda kwenye uchaguzi wa 2024 na 2025 tukiwa na muafaka wa jumla na maelewano yanayokidhi uchaguzi huru na wa haki," alisema. Kuhusu Katiba Mpya Katika majibu yake hayo kuhusu swali la Katiba Mpya, Kinana alisema msingi wa mchakato huo ni kutojifunga kwenye waraka wowote, yaangaliwe mema ya Katiba iliyopo, maoni ya Katiba pendekezwa na maoni mengine. Katika mchakato huo, Kinana alieleza asasi za kiraia zitashirikishwa na nyaraka nyingine zote muhimu zitazingatiwa. Alisema maoni mazuri yanatolewa, tahadhari na hofu ni vema sektretarieti ikaandaa maazimio mazuri ili yawasilishwe serikalini. Hata hivyo, alikiri kukua kwa Demokrasia nchini, ingawaje kulikuwepo hitilafu katika miaka michache iliyopita. Hoja yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, kulikuwepo na ongezeko kubwa la wawakilishi kutoka vyama vya upinzani na ingeendelea hivyo hata mwaka 2020 kama uchaguzi ungekuwa kama ilivyokuwa nyuma. Akiendelea kujenga hoja hiyo kwa kukiri mapungufu ya kisheria na usimamizi wake. Kuhusu Katiba Mpya, Kinana alisema pamoja na kuundwa tume mbalimbali na kupendekeza mabadiliko ya Katiba, lakini hayakuwahi kutekelezwa. Lakini, alisema katika Serikali ya awamu ya sita, angalau ameona dalili za kuwepo kwa mabadiliko ya Katiba. Kwa sasa, alisema kuna michakato ya namna ya kuipata Katiba, kadhalika mchakato mwingine unaendelea wa mabadiliko ya sheria za uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025. "Sheria hizi zitatazamwa upya ili kujibu matakwa ya demokrasia, nina hakika zikitazamwa na wote tukikubaliana na kupelekwa bungeni kwa namna tulivyokubaliana tutakuwa na uchaguzi huru na haki kuliko wakati wowote nchini Tanzania," alisema. "Lakini ukiniuliza je, demokrasia imekuwepo naam imekuwepo, je, kuna kasoro naam kasoro zipo ndiyo maana tunakutana humu ndani na tunakutana kupitia baraza la vyama vya siasa," alisema. Hata hivyo, Kinana aliweka wazi kuwa haamini kwamba ili kubadilisha sheria za uchaguzi kunapaswa kupatikana Katiba Mpya. "Kwa mfano tukisema tunataka kubadilisha sheria ya uchaguzi wakati imejieleza kwenye Katiba mnaweza kufanya mabadiliko kwenye sheria hiyo ikapigiwa kura kwenye Bunge na ikafutwa kwenye Katiba na ikabaki iliyopo," alisema. Mtazamo wa Kinana kuhusu Katiba Mpya ilikinzana na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliyesema si tamanio lake kusikia mjadala unaojikita kwenye nchi ilipotoka na ilipo kwa kuwa hayo tayari yameshajadiliwa na yanajulikana. Hoja yake hiyo inatokana na alichoeleza, Katiba iliyopo ilitengenezwa kwa mfumo wa chama kimoja na ukurasa mpya wa kuandika Katiba Mpya ulianza mwaka 2012 lakini ulikwama 2014. Kwa sababu ya mkwamo huo na kuchelewa kukwamuliwa, Mnyika alisema ni muhimu kuandika Katiba Mpya sasa kama msingi wa mabadiliko ya sheria mbalimbali. Lakini, alieleza masikitiko yake kwa ahadi iliyowabi kutolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Januari kuundwa kwa kamati za mchakato wa mabadiliko hayo lakini hadi sasa hazijaundwa. "Nisikitike pia, hivi karibuni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro ametoa kauli kwamba mchakato utaanza Septemba (mwaka huu) kwa kutoa elimu kwa wananchi, jambo ambalo lilishafanyika, njia hii si sahihi," alisema. Kwa kuwa maoni yameshatolewa, alisema ni muhimu kutafuta muafaka ili katika mkutano wa Bunge wa Septemba upelekwe bungeni muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba. Hoja yake ya pili, alisema kwa sababu mchakato wa Katiba Mpya umechelewa, kunapaswa baada ya kupitishwa kwa sheria, vyombo vya awali vitakavyopitishwa vianze na sheria za masuala ya uchaguzi. "Kukishajengwa muafaka kwenye eneo la uchaguzi, haraka sana yafanyike marekebisho kwenye maeneo hayo, sisi tulishaainisha maeneo hayo. "Nasisitiza kwamba ni vigumu kujihusisha na sheria bila kuanza na mabadiliko ya Katiba ama kwa ujumla wake au marekebisho ya baadhi ya vifungu," alisema. Hali ya Demokrasia Katika mjadala huo, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Juma Duni Haji alisema iwapo ataulizwa kuwa Tanzania ina Demokrasia au laa, atajibu iliyopo ni ndogo mno. "Tatizo tulilonalo ni kwamba demokrasia yetu imemilikiwa na Dola, tunaitazama CCM lakini hata yenyewe ingekuwa kama sisi ingelalanika," alisema. Alieleza vigezo vya Demokrasia ni watu kuwa huru, kuwa na Serikali iliyochaguliwa na watu kwa ajili ya watu na kuwepo vyombo vinavyolinda uhuru wa watu. "Hatujawa huru kuichagua Serikali tunayoitaka tukiwa huru, bahati mbaya sheria tumefungia wenyewe na Katiba tumetunga wenyewe lakini hatuzifuati," alisema. Alieleza kama Tanzania ipo tayari kuwa na demokrasia sheria zinazotungwa kuendesha uchaguzi alisema zinapaswa kufuatwa. "Hivi sasa bado sheria zetu, angalau mwaka huu zimalizike ili angalau itakapotoka uchaguzi wa Serikali za Mitaa tuwe na uchaguzi huru," alieleza. Hata hivyo, alisema tatizo la Tanzania ni kukosekana utashi wa kisiasa kwani makongamano lukuki yanafanyika bila utekelezwaji. "CCM tangu mwanzo hawakuwa wanataka vyama vingi na muda wote wanasimama kuhakikisha CCM inabaki madarakani wengine wanashindwa," alieleza. Alieleza kama taratibu zitafuatwa inawezekana kwa wawakilishi wa vyama vyote vya siasa nchini wawepo bungeni. Alieleza ingawa kutafanyika mabadiliko ya sheria lukuki, lakini hazitafaa kama hakutakuwa na utashi wa kufuatwa na kutekelezwa. "Unaweza kusema ibadilishwe yote, Bunge ni la CCM. Tukisema tusubiri mabadiliko ya Katiba ndiyo sheria za uchaguzi wakikataa tutashindwa," alisema. Kasoro katika tume Akichangia mjadala huo, Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Joseph Selasini alieleza kwa mfumo wa tume ya sasa, uchaguzi unasimaniwa na watu ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). "Tumekuwa na chaguzi lakini zimekuwa kama kiini macho kuonyesha tuna Demokrasia, lakini hazibebi utashi wa wananchi," alisema. Alieleza demokrasia imekuwa ikiingiliwa kwani wanaoshiriki uchaguzi wanajikuta kwenye mateso ya vipigo kutoka katika vyombo vya dola. "Hatuwezi tukaingia kwenye uchaguzi, chama fulani kina mabilioni ya fedha, kingine kina mamilioni ya fedha alafu kuna ambacho hakuna kitu kabisa," alisema. Alieleza ni vigumu kueleza kuhusu demokrasia ilhali vipo baadhi ya vyama visivyo na uwezo wa kufanya safari hata ya kilomita chache za kwenda kuelimisha jamii kuhusu demokrasia. "Watu wengi wana uwezo wa uongozi, lakini wanashindwa kuingia kwa sababu hawamudu gharama za kutafuta uongozi, tulifanya hivi tutaendelea kuwa na viongozi matajiri na wale wengine watabaki kama walivyo," alieleza. Akijibu kuhusu maana ya tume huru Selasini alisema ni mlolongo mzima wa tume husika kuanzia juu hadi chini. Alichopendekeza ni kuwepo chombo huru kitakachopendekeza kwa njia ya mahojiano watu ambao Rais atawateuwa kuingiza tume. Baada ya kuteuliwa, alieleza wao ndiyo wanapaswa kuandika kwamba nani anataka awe msimamizi wa uchaguzi eneo fulani na waajiriwe kuifanya kazi hiyo. "Tunapozungunza uchaguzi mkuu mwanzo wake ni uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hausimamiwi na sheria za uchaguzi bali unasimaniwa na Tamisemi," alisema. Rungwe na uhuru wa kuzungumza Akichagia mjadala huo, Mwenyekiti wa chama cha Chauma, Hashim Rungwe alisema uhuru wa kuzungumza unaanzia tangu binadamu anapozaliwa. "Binadamu kama hatakuwa na uhuru wa kuzungumza ujue ni matatizo katika jamii yenu ama nyumbani au katika taifa, lakini binadamu ameumbwa ili awe na fikra," alisema. Alieleza kila mtu anapaswa awe na uhuru wa kuzungumza isipokuwa asikiuke mipaka, mathalan kutoa lugha za matusi. Kwa mujibu wa Rungwe, wananchi wa Tanzania wamekuwa na uwoga wa kuzungumza wakidhani watafuatwa na vyombo vya dola, hivyo uhuru walionao umekuwa na mipaka. "Uhuru huu una mipaka yake, nimetoa kama ufupisho, lakini nafikiri Watanzania kwa ujumla wetu tuna haki ya kuzungumza hasa mambo yanayotukera, lazima uzungumze ili Serikali itusikie," alisema. Akijibu hoja kuhusu hali ya Demokrasia, Makamu Mwenyekiti wa CUF, Maftah Chuma alisema ni mbaya kwa sababu ya mifumo iliyopo. "Vyombo vinavyohusika na kusimamia uchaguzi mwaka 2020 vilidhamiria kutumika kuharibu uchaguzi huo, vyombo vya dola vilifanya kazi kubwa ya kuharibu uchaguzi ambao upo kwa mujibu wa sheria," alisema. Alisema hayo yanafanyika wakati sheria mbalimbali zinazosimamia kufanyika kwa uchaguzi zipo.
Kama ni umri wa binadamu, unaweza kusema amebakiza miaka mitano kustaafu, huu ndiyo uhalisia wa miak
Kama ni umri wa binadamu, unaweza kusema amebakiza miaka mitano kustaafu, huu ndiyo uhalisia wa miaka liliyonayo Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), lililoanzishwa Juni 19, 1963. Kanisa hilo ambalo mwaka huu, linatimiza umri wa miaka 60 tangu lilipoanzishwa, msingi wa kuanzishwa kwake ni muungano wa makanisa saba ya Kilutheri na kuunda KKKT. Kwa mujibu wa Mkuu wa Kanisa hilo, Askofu Frederick Shoo makanisa hayo saba yaliyoungana ni Kanisa la Kilutheri la Iraqw, Kanisa la Kiinjili la Tanganyika ya Kaskazini Magharibi na Kanisa la Kilutheri la Tanganyika ya Kaskazini. Mengine ni Kanisa la Kilutheri la Tanganyika ya Kati, Kanisa la Kilutheri la Tanganyika ya Kusini, Kanisa la Kilutheri la Uzaramo-Uluguru na Kanisa la Kilutheri la Usambara-Digo. Jana, Kanisa hilo liliadhimisha miaka 60 ya kuanzishwa kwake jijini Arusha, huku Askofu Shoo akikabidhi tuzo maalum kwa wazee walioshuhudia utiwaji saini ya uanzishwaji wake. Askafu Shoo alisema wanaopewa tuzo hizo ni Mchungaji Johansen Rutabingwa (96) na Elirehema Mwanga (86), walioshuhudia muungano wa makanisa saba yaliyounda KKKT. Kulingana na mkuu huyo wa KKKT, Mchungaji Mwanga wakati huo alikuwa mwanzilishi wa kanisa la Usambara Digo huku Mutabingwa akiwa mwakilishi wa vijana wakati huo. "Awali yalikuwa makanisa saba yaliyotajwa kwa maeneo na makabila, ndivyo walivyofanya wamisionari. Wazee baada ya kupata uhuru roho mtakatifu akawaongoza kwanini msiwe na kanisa moja la Kilutheri, hawa wazee hapa wao walikuwepo walishuhudia kuwekwa saini kwa makubaliano yake Juni 19, 1963. "Kuna watu hawapendi umoja wa kanisa, hawapendi muungano wanasema sisi ni kanisa moja lakini ni federation ya yale makanisa, mimi nasema huo ni upotoshaji wa makusudi wa historia ya kanisa, sisi ni kanisa moja la KKKT, tunakemea roho ya upotoshaji inayotaka kueneza histori ya uongo," alisema. Hata hivyo, Askofu Shoo alisema kanisa hilo lilianza na waumini 500,000 mwaka 1963 lakini sasa limefikia zaidi ya waumini milioni nane. Kwa mujibu wa Dk Shoo, wakati linaanzishwa lilikuwa na Dayosisi saba, lakini sasa zimeongezeka na kufikia 27 katika Mikoa yote nchini. Si huduma za kiroho pekee, zinazotolewa na kanisa hilo, Askofu Shoo alisema hata zile za kijamii hutolewa pia zikiwemo za afya kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hospitali za Rufaa. “Katika kipindi cha miaka 60 tumeendesha huduma za afya kuanzia ngazi za zahanati hadi hospitali za rufaa, tumechangia katika elimu kuanzia shule za awali, vyuo vya kati, vikuu na elimu ya watu wazima,” alisema Askofu huyo. Huduma nyingine zinazotolewa na kanisa hilo kama sehemu ya mafanikio ya miaka 60 ya kuanzishwa kwake, alisema ni utetezi na kupinga ukatili, kusaidia waathirika wa ukatili au magonjwa, ukatili dhidi ya wenye ulemavu wa ngozi, ukatili dhidi ya wanawake, ukeketaji na haki nyinginezo. “Kwa miaka hiyo tumepitia nyakati tofauti na katika hizo licha ya changamoto tunaendelea kujivunia kanisa linaendelea kukua ni jambo la kumshukuru Mungu kwa ushiriano kati ya Serikali na kanisa,” alisema. Alieleza ushirikiano kati ya Kanisa na Serikali umezingatia ustawi wa wananchi pasi na ubaguzi. Pamoja na mafanikio lukuki, alisema changamoto mbalimbali zinawakabili katika safari hiyo, ikiwemo kutozwa kwa kodi kwenye vifaa vya utoaji huduma na urasimu haswa kwenye madeni na baadhi ya taasisi za Serikali. “Nilikekera juzi mtu mmoja alisema kwanini Serikali inatumia fedha zake kuendesha taasisi za kikristo, watu wamesahau historia ya nchi kwenye mchango wa makanisa na miaka ya 1990 KKKT ilisaidia kuendesha kampeni kwa kushirikiana na wadau iliyohusu Serikali kufutiwa madeni na kampeni hiyo ikafanikiwa na Rais wa kipindi hicho, Benjamin Mkapa alituandikia barua maalum kutambua kazi hiyo njema iliyofanywa na kanisa,” alisema. Hata hivyo, aliishukuru Serikali kwa kutoa Sh5 bilioni kugharimia ujenzi wa jengo la matibabu ya saratani ambao kwa sasa umefikia asilimia 70, katika hospitali ya Rufaa ya KCMC inayomilikiwa na kanisa hilo.
Sakata la uwekezaji bandari linaweza kuwa moja ya mitihani migumu kuwahi kumkabili Rais Samia Suluhu
Sakata la uwekezaji bandari linaweza kuwa moja ya mitihani migumu kuwahi kumkabili Rais Samia Suluhu Hassan tangu aapishwe kushika wadhifa huo. Kulingana na wataalamu wa masuala ya siasa na utawala, sakata hilo limefikia hatua ya hata kuamua imani ya wananchi juu ya Serikali yao, iwapo haitazichanga vema karata zake. Hata hivyo, wanazuoni hao wanasema kuibuka kwa taasisi za kidini kutoa tamko kuhusu sakata hilo, ni matokeo ya vitisho na kuminywa kwa wenye wajibu huo, wakisisitiza Serikali itoe uhuru huo. Pamoja na milima na mabonde aliyopitia Rais Samia tangu alipoapishwa kuwa Rais, Machi 19, mwaka 2021, hili la mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uboreshaji bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia DP World ni kiunzi kisichomithirika. Mkuu huyo wa nchi, aliapishwa kuwa Rais, katikati ya janga la Uviko-19, lakini alivuka salama na baadaye kumwagiwa sifa kwa kustawisha siasa, diplomasia, kuondoa wafungwa wa kisiasa magerezani, kuunda kikosi kazi na baadaye tume ya haki jinai. Katika utawala wake, ndipo ruhusa ya kufanyika mikutano ya hadhara ilipotoka baada ya kuzuiwa kwa takriban miaka saba, lakini ameridhia kuanza kwa mchakato wa mabadiliko ya Katiba. Mtihani wa kwanza kumkabili ulitokana na uamuzi wake wa kuanzisha tozo katika miamala ya simu Juni 2021, lililoibua upinzani mkali kutoka kwa wananchi, kwa kile kikicholalamikiwa kuwa hatua hiyo iliongeza ukali wa gharama za maisha. Baada ya hilo, mchakato wa Katiba Mpya ndiyo ulitazamwa kuwa mtihani mwingine mgumu katika utawala wake, lakini kwa hali ilivyo katika mkataba wa ushirikiano wa uboreshaji na uwekezaji wa Bandari ya Dar es Salaam, kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia kampuni ya DP World, hili limebeba uzito wa aina yake. Msingi wa suala hili kuwa mtihani kwake ni upinzani mkali linalokabiliana nao ambao mbali na ule unatoka kwa wanasiasa wa upinzani ambao aghalabu hupingana na Serikali ya CCM, kwenye sakata la bandari imekwenda mbali zaidi kwani hata viongozi wa dini wanaupinga. Agosti 18, mwaka huu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), lilitoa tamko ililoliita 'Sauti ya Watu, Sauti ya Mungu' likitaka kuondolewa kwa ridhio la mkataba huo kutokana na kupingwa na wananchi, lakini kukiuka baadhi ya sheria za nchi. "Sisi Maaskofu Katoliki Tanzania wenye jukumu la kusimamia ustawi wa kila mwanadamu tunamwomba Rais Samia Suluhu Hassan, kwa mamlaka aliyonayo asitishe wasilisho la ridhio hili kwa upande wa pili na vilevile Bunge nalo lifute ridhio la mkataba huu unaolalamikiwa,” ilieleza sehemu ya tamko hilo, lililotiwa saini na Katibu Mkuu wa TEC, Padri Charles Kitima. Si viongozi wa dini pekee, upinzani huo unahusisha hata wataalamu wa sheria na jumuiya zinazowasimamia kikiwemo Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kilichopendekeza maboresho makubwa ndani ya mkataba huo. Hayo yanafayika, wakati Serikali imeshaingia gharama za uelimishaji wananchi katika Mikoa mbalimbali kuhusu tija ya mkataba huo, lakini haijafua dafu. ‘Mkataba na athari za kisiasa kwa CCM’ Akizungumzia hilo, Mhadhiri Msaidizi wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Revocatus Kabobe alisema kutokana na mwenendo wa sakata hilo, kisiasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaweza kugharimika. “Kisiasa hoja ya bandari inaweza kuigharimu CCM kwenye chaguzi za Serikali za Mitaa (2024) na hata Uchaguzi Mkuu (2025) kama wakipotezea maoni ya wengi ambao kimsingi hawapingi uwekezaji wanataka mabadiliko kwenye huu mkataba,” alisema. Hata hivyo, Kabobe alieleza hisia tofauti juu ya CCM ambayo aghalabu huwa na tabia ya kubadilika kulingana na wakati hasa linapokuja suala lenye mwonekano wa kukipunguzia kura kwenye chaguzi. “Sitashangaa kwenye suala la bandari CCM ikiamua kufuta huo mkataba na kufanya mabadiliko. Naamini bado wanatafakari namna bora ya kuondoa kasoro za huo mkataba bila wao kuonekana wameshindwa,” alisema. Lakini, alisema ili viongozi wawe salama kisiasa lazima wakae upande wa wananchi na si vinginevyo, kinyume na hivyo imani ya umma dhidi yao itapungua kwa kuona unapuuzwa. “Ili kwenda sawa ni vizuri masuala kama haya ya mikataba inayogusa rasilimali za nchi ifuate sheria na maoni ya wananchi kabla ya kufanyiwa maamuzi na viongozi,” alisema. Kwa upande mwingine, Kabobe alisema mkataba huo ni mtaji kwa wapinzani wa CCM maana wanatumia hoja hiyo kushambulia katika majukwaa ya kisiasa. Hoja ya Kabobea inaungwa mkono na Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Matrona Kabyemela aliyesema katika mfumo wa demokrasia wananchi ndiyo wenye mamlaka ya kumuongoza Rais, wanapoona anapotoshwa au kwenda kinyume na Katiba. “Mimi kwanza namshukuru Rais kwa kuwa amefungua uhuru wa kutoa maoni na hivyo natumaini atayachukua maoni kwa mtazamo chanya na kuyafanyia kazi. “Kwakuwa wanachi ndo waajiri wa viongozi wa kisiasa basi viongozi hawana budi kupitia kwa umakini maoni yanayotolewa ili yale yanayojenga yafanyiwe kazi,” alisema. Lakini, alisema mkataba unaweza kuboreshwa kwa hekima ya kuchukua mawazo mazuri kwa kuwa pia kuna yanayopotoshwa ndani yake. Mhadhiri Msaidizi kutoka chuo hicho, Sabatho Kabyemela alisema ugumu wa mtihani huo, unatokana na mjadala wa mkataba huo kutanua nyufa katika taifa. “Nyufa zilizojitokeza zina sura za utaifa finyu yaani uzanzibari dhidi ya utanganyika, udini yaani ukristo dhidi ya uislamu na matumizi ya mabavu ya dola dhidi ya wananchi wanaokosoa mkataba huo,” alisema. Alisema nyufa hizo hazina dalili njema kwani zisipozibwa zitasababisha mpasuko hasa katika kipindi ambacho nchi inaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024 na uchaguzi mkuu wa 2025. “Tusipokuwa makini, mjadala wa bandari utaligawa taifa katika vipande vipande katika chaguzi zijazo na mpasuko huo utaendelea kulitafuna taifa hadi litakapomalizika. Ni vema wanaong’ang’ania mkataba huu wajiulize: Je, wapo tayari kuendelea nao kwa gharama ya umoja na mshikamano wa kitaifa?,” alihoji. Lakini, alisema kuibuka kwa matamko ya taasisi za kidini, ni matokeo ya matumizi ya dola kunyamazisha sauti mbadala zilizopaswa kutolewa kupitia mijadala ya wazi. Kwa mujibu wa Kabyemela, kumekuwepo na mazingira ya nguvu inayotumiwa na dola na wanaoiunga mkono, kunyamazisha wale wanaopinga mkataba husika. “Nguvu hiyo imeonekana katika matumizi ya propaganda, vitisho, uzuiaji wa maandamano na hata ukamataji wa wapinzani wa mkataba. Vilevile kumekuwa na mashambulizi yenye sura ya ubaguzi wa kidini na hata kimbari yaliyoelekezwa kwa wanazuoni waliokosoa mkataba huo,” alisema. Nguvu hiyo, alisema ndiyo sababu ya kutokuwepo kwa mijadala ya kina katika taasisi za kiraia kama jumuiya za wanataaluma na vyama vya wafanyakazi kuhusu mkataba huo. “Ni katika hali kama hiyo ndiyo tunapoona maaskofu wa kikatoliki wakiibuka na waraka wa kuweka msimamo juu ya mkataba huo,” alisema. Kwa bahati mbaya, alisema yanayozungumzwa na kutendwa na wasaidizi wa viongozi, hayaonekani kuwa na afya katika mjadala unaoendelea. “Binafsi nawahurumia sana viongozi wetu wa kitaifa maana nadhani hawawezi kuelewa joto lililoko huku mtaani. Kwa ukubwa na uwingi wa majukumu yao ni vigumu kuelewa kinachoendelea kwa wananchi wa kawaida, kwa maana hiyo wanategemea zaidi ushauri kutoka kwa wasaidizi wao. “Kwa bahati mbaya, yanayozungumzwa na kutendwa na wasaidizi wa viongozi wetu hayaonekani kuwa na afya katika mjadala unaoendelea na mustakabali kwa taifa na badala yake yanaongeza mgawanyiko zaidi,” alisema. Ili kuondokana na mkwamo uliopo sasa, alipendekeza mambo matatu yafanyike. Alitaka kusitishwa kwa matumizi ya nguvu na vitisho kwa wakosoaji wa mkataba kwa sababu sio afya kwa taifa linaloendeshwa kwa misingi ya kidemokrasia. “Matumizi ya nguvu hayawezi kunyamazisha upinzani dhidi ya mkataba bali yanachochea moto zaidi. Kupinga msimamo wa Serikali kwa kauli au hata kwa kusudio la maandamano sio uhaini bali ni haki zilizoainishwa katika Katiba. Viongozi wasiwaamulie wananchi jinsi gani wanataka kupingwa. Wananchi wataamua wenyewe kulingana na mwongozo uliowekwa katika katiba,” alisema. Pia, alitaka kusitishwa kwa mkataba husika ili kuepusha mgawanyiko ulioibuka. “Baadhi ya wasaidizi wa viongozi wetu wanashauri Serikali ikaze shingo katika mkataba huu kwani ikibadili uamuzi wake itaonyesha haina msimamo na hivyo kuzidi kumomonyoa imani waliyonayo wananchi kwa viongozi wao. Mtazamo huu ni hatari sana kwani unailazimisha Serikali kupuuza maoni ya wananchi,” alisema. Kingine alichokipendekeza ni kuwepo na mjadala wa kitaifa juu ya mwelekeo wa uchumi wa nchi, wajibu wa dola katika uchumi na nafasi ya wananchi katika kufaidika na rasilimali zao. “Kwa bahati nzuri tunao uzoefu wa kutosha wa uwekezaji kutoka ughaibuni nchini, ulioelekezwa katika sekta mkakati kama uzalishaji wa nishati, uchimbaji wa madini, uendeshaji wa mashirika ya umma, ubinafsishaji wa viwanda. “Kote huko uwekezaji haukufanya vizuri bali ulisababisha ufisadi mkubwa, upandaji wa gharama za huduma, upotevu wa mapato ya Serikali, upotevu wa ajira na kufungwa kwa viwanda,” alisema. Uzoefu huo, alieleza unatosha kuwakumbusha Watanzania kuwa wana wajibu wa kuendesha sekta mkakati za kiuchumi wenyewe na ndilo takwa la maaskofu katika tamko lao. Hata hivyo, alisema pamoja na kukubaliana na yaliyomo kwenye tamko la TEC, lakini lilipaswa kutolewa na vyama vya ushirika, vyama vya wafanyakazi, vyama vya wanataaluma na asasi za kiraia. “Kwa bahati mbaya, kama nilivyodokeza, kutokana na vitisho vinavyotolewa na dola, vyombo vya kiraia na kuacha ombwe ambalo limezibwa na vyombo vya kidini. Ni vema kuwa na mjadala wa kina juu ya nafasi ya vyombo vya kidini na vyombo vya kiraia visivyo vya kidini katika mijadala ya kitaifa katika nchi yetu,” alisema. Alisema iwapo wigo wa vyombo vya kiraia utatanuliwa, basi vyombo vya kidini vitajikita katika masuala ya kiroho na kuacha yenye muelekeo wa kisiasa katika vyombvo vinavyostahili.
Hatimaye rasimu ya maboresho ya mitalaa na sera ya elimu imezinduliwa na kuzua mjadala kutoka kwa wa
Hatimaye rasimu ya maboresho ya mitalaa na sera ya elimu imezinduliwa na kuzua mjadala kutoka kwa wadau wa sekta hiyo, baadhi wakipongeza wengine wakilalamikia kurejewa kwa mambo nayoyapinga. Miongoni mwa mambo hayo ni lugha ya Kiingereza kutumika kufundishia kuanzia ngazi ya sekondari hadi elimu ya juu, wakitaka kitumike Kiswahili ili kujenga maarifa zaidi. Rasimu hizo zimezinduliwa juzi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolfu Mkenda jijini Dodoma, zikitarajiwa kuwa muarobaini wa changamoto ya ubora wa elimu nchini. Kulingana na rasimu ya sera, elimu ya awali itatolewa kwa mwaka mmoja, ya msingi kwa miaka sita, kadhalika kila mwanafunzi atafika kidato cha nne bila kikwazo cha mtihani wa darasa la saba. Katika rasimu ya mtalaa, mbali na kuongezeka kwa somo la historia ya Tanzania na maadili litakalofundishwa kwa Kiswahili katika ngazi zote za elimu, masomo ya lugha yameongezeka ikiwemo, Kiarabu, Kichina na Kifaransa. Imerudia makosa Akizungumza na gazeti hili, Mhadhiri wa Lugha kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Dk Aginiwe Sanga alisema rasimu hiyo imetegua kitendawili cha lugha rasmi ya kufundishia kinyume na ilivyotarajiwa na wengi. “Tumepigania muda mrefu sana tukitaka Kiswahili kitumike kufundishia kuanzia ngazi ya msingi hadi elimu ya juu, lakini bado hatufikii muafaka, imerudia makosa yale yale,” alisema. Kwa mujibu wa rasimu hiyo ya sera, lugha ya Kiswahili itatumika kufundishia katika elimu ya awali na msingi, isipokuwa masomo ya lugha za kigeni na katika shule zitakazoomba kutumia lugha ya Kiingereza. Kadhalika, rasimu hiyo inafafanua Kiingereza kitatumika kufundishia kuanzia ngazi ya sekondari ya chini, isipokuwa somo la Kiswahili, masomo ya lugha za kigeni na katika shule za sekondari na vyuo vitakavyoruhusiwa kutumia Kiswahili kufundishia. Shinikizo la kutumika Kiswahili Dk Sanga, alisema linatokana na ukweli kwamba lugha hiyo ndiyo asili ya mtanzania hivyo itarahisisha kunasa maarifa iwapo itatumika kumfundishia. “Nadhani kuna ushawishi au uoga unaowafanya viongozi wa Serikali kushindwa kuamua hili, maana sioni sababu ya moja kwa moja kwamba kwanini Kiswahili kisitumike katika hilo,” alisema. Alisisitiza kuwa Serikali imefanya juhudi mbalimbali za kuwekeza katika umahiri wa lugha hiyo na hatimaye inatambulika ulimwenguni, kwanini isitumike kufundishia. Watahitimu na umri mdogo Rasimu hiyo inatamka kuwa, elimu ya msingi itaishia darasa la sita na umri wa kuanza darasa la kwanza ni miaka sita, jambo lililotajwa na Dk Zubeda Mussa mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE), kuwa litazalisha wahitimu wenye umri mdogo zaidi. Athari yake, alisema ni kushindwa kujisimamia wanapofikia ngazi nyingine za elimu kwa kuwa umri wao hauwawezeshi kupambanua mazuri na mabaya. “Kutokana na ulimwengu ulivyo kwa sasa naona kama tunawawahisha sana watoto, kwa sababu anaanza darasa la kwanza akiwa na miaka sita akiingia sekondari hawi na uwezo wa kujisimamia,” alisema. Alisema angalau kungekuwa na kigezo cha kuanza darasa la kwanza wakiwa na umri wa miaka saba, ili wahitimu elimu ya msingi wakiwa wamepevuka. Maoni ya Dk Zubeda, yanatofautiana na Mtafiti na mchambuzi wa masuala ya elimu, Muhanyi Nkoronko aliyesema utaratibu huo utatoa wigo mpana kwa watoto kuyafikia malengo yao ya kielimu mapema. “Huu wa sasa unamfanya mtoto achelewe kuyafikia malengo yake ya kielimu, lakini kama ataishia darasa la sita maana yake atahitimu akiwa na umri mdogo na hatimaye kufikia malengo mapema,” alisema. Rasimu hiyo ya sera pia inatamka kutoa nafasi kwa kila mwanafunzi kufika sekondari, jambo ambalo Nkoronko alisema linatoa wigo mpana kwa watoto kufikia kiwango hicho cha elimu. Alipoulizwa iwapo hatua hiyo haitashusha thamani ya elimu ya sekondari, Nkoronko alisema rasimu imetaja mbinu mbalimbali zitakazotumika kujenga maarifa kwa muhitimu wa sekondari ili awe na hadhi na uelewa kulingana na mazingira. Pamoja na mazuri hayo, Nkoronko alieleza hofu aliyonayo juu ya utekelezwaji wa sera hiyo itakapopitishwa kwa kuwa utahitajika uwekezaji mkubwa wa miundombinu. “Wakati wale wahitimu wa darasa la saba wanamaliza kwa sera hii ya sasa, watahitimu mwaka mmoja na hawa wa nyuma yao ambao sera inayokuja inawataka kuishia darasa la sita. “Kwa msingi huo hawa wataingia sekondari mwaka mmoja, tutakuwa na makundi mawili yanayohitimu yote yakihitaji miundombinu ya madarasa na samani na mambo mengine sekondari,” alisema. Alieleza wakati Serikali inaliendea suala la maboresho hayo, mitalaa katika vyuo vya ualimu isisahaulike ili kutengeneza uwiano na kuandaa rasilimaliwatu itakayoendana na mabadiliko ya sasa. Yaendane na maboresho ya sheria Maboresho hayo yatakuwa na tija zaidi iwapo yataendana na marekebisho ya baadhi ya sheria, kanuni na taratibu zinazoisimamia sekta ya elimu kama inavyoelezwa na mdau wa sekta hiyo, Dk Ave-Maria Semakafu. Hilo linatokana na kile alichokifafanua kuwa, kumekuwa na mkanganyiko katika sheria hizo, hali inayokwamisha utekelezaji wa baadhi ya mambo kwenye sekta ya elimu. “Tunapokuja na maboresho hayo ni vema kujua, uendeshaji wa shule kwa sasa unafanyikaje, shule zitakuwa mali ya Wizara ya Elimu au Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),” alisema Dk Semakafu aliyewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu. Kwa mujibu wa Dk Semakafu, ugatuzi wa madaraka ya usimamizi wa shule kutoka Wizara ya Elimu hadi Tamisemi, ulifanyika pasi na mabadiliko ya sheria. Hali hiyo, alieleza inayumbisha utendaji wa baadhi ya viongozi katika sekta hiyo, ikiwemo nafasi ya Kamishna wa Elimu. “Shule zipo chini ya Tamisemi, Kamishna wa Elimu anatokea Wizara ya Elimu kuna wakati akitoa maelekezo Waratibu wa Elimu wanapata mkwamo wa kuyatekeleza kwa kuwa wameshapokea mengine kutoka Tamisemi,” alisema.
Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia katika ngazi zote za elimu, kimeendelea kuwa kitendawili kisicho
Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia katika ngazi zote za elimu, kimeendelea kuwa kitendawili kisichoteguka, licha ya mijadala ya muda mrefu ya kulishinikiza hilo. Huu ni mwaka wa 55 sasa tangu mijadala kuhusu Kiswahili kitumike kufundishia ngazi zote za elimu ianze, lakini bado haijawahi kuzaa matunda. Matumaini ya wadau wa elimu kuhusu lugha hiyo kutumia kufundishia ngazi zote za elimu, yalibaki kwenye kitakachoelezwa na rasimu ya sera ya elimu inayoendelea kujadiliwa sasa, lakini matokeo yakawa kinyume chake. Kwa mujibu wa rasimu ya sera hiyo, asilimia 72 ya wadau waliohojiwa, wamependekeza Kiingereza liendelee kutumika kufundishia kwa elimu ya Sekondari ya chini na kuendelea. Lugha ya Kiswahili, rasimu hiyo imetamka itatumika kufundishia elimu ya awali na msingi, jambo ambalo halina tofauti na inavyotekelezwa sasa. Hata hivyo, rasimu hiyo imetamka shule za Sekondari zitakazoruhusiwa pekee ndizo zitakazotumia Kiswahili kufundishia, ingawa haikubainisha vigezo. Kilichopendekezwa katika rasimu hiyo, kinatajwa kutokidhi matarajio ya wadau wa elimu, kama anavyoeleza Mtunzi wa vitabu, Mwalimu Richard Mabala. Kwa miaka mingi, anasema lugha hiyo inapendekezwa kutumika kwa ajili ya kufundishia katika ngazi zote za elimu, lakini uamuzi unakwaa kisiki. "Sijui kwanini hata tafiti zilizofanyika na kueleza kuwa Kiswahili kinafaa kitumike, lakini zinapuuzwa," anaeleza. Kulingana na Mwalimu Mabala, katika rasimu hiyo imeelezwa shule za sekondark zitakazoruhusiwa pekee ndizo zitakazotumia Kiswahili, akihoji kwa kigezo gani. Hoja nyingine alinayoibua katika hilo, wanafunzi wa shule hizo watatahiniwa kwa lugha gani na veyti vyao vitafanana na vya wengine walizosoma sekondari kwa Kiingereza. "Bado rasimu imeacha maswali mengi, tukitarajia ingeweka wazi moja kwa moja kwamba Kiswahili ndiyo kitumike kufundishia katika elimu yote nchini," anasema. Ingawa kuna faida na hasara za kukitumia Kiswahili kufundishia ngazi zote za elimu, mhadhiri mwandamizi katika saikolojia ya elimu na mafunzo ya mitalaa kutoka Chuo Kikuu Kushiriki cha Elimu (DUCE), Dk Florence Kyaruzi anasema kunahitajika maandalizi kabla ya kufikia huko. Anayataja maandalizi hayo ni rasilimaliwatu watakaotekeleza hilo, kutafsiriwa kwa vitabu kwa kuwa vyote vipo katika lugha ya Kiingereza. "Kuna haja ya kufanya maandalizi ya kutosha, Kiswahili kikitumika ngazi zote litakuwa jambo jema lakini inahitajika miundombinu ili hilo liwezekane. "Tuwe na walimu wenye uwezo wa kufundisha masomo haya kwa Kiswahili kuanzia ngazi ya chini hadi juu," anasema. Anasisitiza ingefaa iwapo Kiswahili kingetumika kufundishia, lakini kunahitajika maandalizi. Anazitaja faida za kukitumia Kiswahili ni kile kilichowahi kuelezwa kwenye tafiti nyingi kwamba, mtu atajifunza vizuri iwapo atatumia lugha yake ya kwanza. Anasema hiyo haimwezeshi kufaulu tu, bali inamfanya kuelewa kwa kina kile anachojifunza, badala ya kukariri. "Kama watu watajifunza kwa lugha zao, utawafanya wawe na uwezo wa kudadisi, kujadili na kushirikiana," anasema. Lakini upande wa hasara, anafafanua Kiingereza kinatumika na mataifa mengi duniani, ni kama lugha ya biashara. "Watu wanaona mtoto akijifunza kwa Kiswahili atabobea kwenye lugha hiyo na kushindwa Kiingereza, lugha ambayo unatumika kimataifa," anaeleza. Dk Kyaruzi anasema Kiingereza pia ndiyo lugha yenye eneo kubwa la watumiaji na inatawala uchumi wa ulimwengu ni vema kuifahamu. Kuhusu kilichopendekezwa kwenye rasimu hiyo, Dk Kyaruzi anasema kuna haja ya kujua kwanini asilimia zaidi ya 70 ya watoa maoni wametajwa Kiingereza kuanzia ngazi ya Sekondari ya chini. Wanachokisema wanafunzi Wasomi nao wanapendekeza Kiswahili kitumike kufundishia katika ngazi zote za elimu, wakifafanua kufanya hivyo ni kutekeleza falsafa ya kujitegemea, kwa mujibu wa Maria, Rais wa Shirikisho la Vyuo Vikuu Tanzania (TAHLISO). Anasema nchi nyingi ikiwemo Tanzania zinajitegemea kwa lugha, si vibaya ikatumika kufundishia, utatafsiri kujitegemea huko. "Huwezi ukaenda Marekani ukakuta wanafundisha kwa Kiswahili, vivyo hivyo China na mataifa mengine, ufike wakati nasi tufundishe kwa Kiswahili," anasema. Kwa mujibu wa Maria, maendeleo ya taifa lolote huchagizwa na uwezo wa nchi husika kujitegemea juu ya kile ilichonacho. "Ni vema tutumie Kiswahili sasa kufundishia katika ngazi zote za elimu kama litawezekana, kwa sababu ndiyo lugha yetu," anaeleza. Wakati wengine wakipendekeza hayo, Mwalimu kutoka Shule ya Sekondari Sunshine, Concheska Kilama anasema utaratibu uendelee kama ilivyopendekezwa kwenye rasimu. Hoja yake hiyo inatokana na kile anachoeleza kuwa, Kiingereza no lugha ya kimataifa hivyo, kikitumika kutarahisisha wasomi nchini kuvuka mipaka ya nchi. "Pia inakua rahisi sisi kushirikiana na watu wa mataifa mengine kupitia lugha na hivyo kupanua wigo na kukua kibiashara na hata kielimu," anasema. Anasema kitakapotumika Kiswahili, kutawekwa mipaka hasa kwa kizazi kijacho katika ujifunzaji na kupata uzoefu kutoka mataifa mengine. "Tukitumia Kiswahili wanafunzi watakijua Kiswahili na si lugha nyingine, hatutakuwa na uwezo wa kushiriki mambo mbalimbali ya kimataifa," anasema.
Safari ya mabadiliko ya sekta ya elimu imepitia milima na mabonde, huku kila awamu ikikumbana na upi
Safari ya mabadiliko ya sekta ya elimu imepitia milima na mabonde, huku kila awamu ikikumbana na upinzani wake. Mabadiliko ya sekta hiyo, yalianza baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, yakilenga kuvua minyororo ya wakoloni walioitoa elimu kwa maslahi yao. Historia ya mabadiliko ya elimu nchini, ilitokana na malengo ya wakati husika mbali na ile ya kibaguzi iliyokuwa inatolewa kabla ya uhuru iliyolenga kumfanya mtu kuwa mzalishaji kwa nchi yake. Kwa kadri dunia ilivyobadilika, haja ya maboresho ya sekta ya elimu ilionekana na kila mabadiliko yalikuwa na umuhimu wake. Yaliwahi kufanyika mabadiliko yanayoplenga kujenga uwezo wa mwanafunzi kujua kusoma na kuandika, lakini yapo yaliyolenga kumjengea mwanafunzi uelewa. Mabadiliko ya mwisho, yalikuwa katika miaka ya 2010 hadi 2014 yaliyohusisha kushushwa kwa viwango vya ufaulu mitihani ili kupata wanafunzi wengi wanaojiunga na elimu ya sekondari za Kata. Mabadiliko yale yale ya mahitaji ya ulimwengu na kukua kwa sayansi na teknolojia ndiyo yaliyoibua haja ya maboresho ya sekta ya elimu mwaka 2022, yanayoendelea sasa. Kitendo cha mwanafunzi kujengewa uelewa wa anachofundishwa kilionekana si muhimu tena katika mazingira ya sasa na ujuzi umechukua nafasi kama msingi muhimu katika elimu ya kizazi cha leo. Kutokana na mazingira ya sasa haja ya wadau ni kuzalisha wasomi watakaokuwa na ujuzi utakaowawezesha kujitegemea. Katika kufanikisha hilo, Serikali iliunda kamati ya maboresho ya sera na mtalaa wa elimu kwa ngazi zote ili kumfanya muhitimu wa ngazi yoyte awe na ujuzi utakaomwezesha kumudu kujitegemea. Huo ndiyo mzizi wa kuundwa kwa kamati iliyoongozwa na Profesa Makenya Maboko iliyolenga kukusanya maoni ya wadau ili kuboresha sekta ya elimu. Hata hivyo, hatua ya kuundwa kwa kamati hiyo pia, imetokana na msukumo wa Rais Samia Suluhu Hassan, tangu Aprili 6 mwaka juzi alipoagiza kufanywa maboresha katika mitalaa ya elimu. Kauli hiyo, aliirudia Aprili 22, mwaka huo alipotaka maboresho hayo yalenge kujenga mhitimu atakayekuwa na ujuzi. Gazeti la Mwananchi limefanya mahojiano maalum na Profesa Maboko, kujua safari yote ya kukusanya maoni na msingi wa walichokipendekeza juu ya maboresho ya sekta ya elimu nchini, kama yanavyosomeka hapo chini. Mlikutana na wadau gani kwenye kukusanya maoni na mliwachagua kwa vigezo vipi? Sisi tulijitahidi kukutana na wadau wote, kuanzia wazazi, wanafunzi, walimu, viongozi wa siasa, wa dini, watu wa sekta binafsi kundi kubwa sana tulikutana na watu zaidi ya 200,000. Lakini ilikuwa sio lazima ukutane na sisi ana kwa ana uliweza kutoa maoni yako kupitia mtandao, kwa hiyo kila aliyetaka kutoa mawazo alipata fursa ya kufanya hivyo. Kwa kiasi gani mapendekezo yenu yanaakisi maoni ya Rais Samia Suluhu Hassan juu ya kutoa elimu inayojenga ujuzi zaidi kwa wanafunzi? Hata kabla hatujafika nusu ya kukusanya maoni, tulibaini kwamba maoni mengi yalijirudia na hoja kuu ilikuwa kutaka itolewe elimu inayojenga ujuzi wa kumwezesha muhitimu kujitegemea anapomaliza. Unaweza kusema Rais Samia aliwasoma matakwa ya raia wake kwa hiyo mapendekezo yote na sisi imetufurahisha, kwamba huwezi kumridhisha kila mtu kuna watu hawataki kubalidika wanataka lugha fulani itumike mahali fulani lakini ukiwaweka kwenye mizania unakuta asilimia ngapi wanataka hiki utapata majibu. Kwa ufupi mapendekezo yote yanaakisi kwa kiwango kikubwa maono ya Rais. Mnaridhishwa na kasi ya maandalizi ya utekelezaji wa mapendekezo yenu? Kasi inaridhisha kwa sababu mpango ulivyo hatuanzi na mitalaa yote ya shule zote, tumegawa mfumo wote wa elimu katika makundi sita, tutaanza na darasa la awali na wale wa la kwanza. Kwa maana kwamba darasa la pili wtaendelea na mtalaa wa zamani hadi watakapomaliza darasa la saba, pia tutaanza na wanafunzi wa darasa la tatu kwa mtalaa mpya, lakini wale wa darasa la nne wataendelea na mtalaa wa zamani. Vile vile tutaanza na wanafunzi wa kidato cha kwanza na wale wa kidato cha tano. Baadhi ya maandalizi yamewekwa kwenye tovuti za elimu na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) ambaye ndiye msimamizi, inaandaa bajeti ya kuanza kuandaa vifaa na utaratibu wa mafunzo kwa walimu. Kulikuwa na mapendekezo ya elimu ya amali, hii inatofautiana vipi na elimu ya ufundi? Elimu ya amani, mwanzoni tulikuwa tunatumia neon ufundi lakini kihistoria ukisema ufundi hapa kwetu kila mtu anajua ufundi nyumba, seremala, magari. Sasa neon amali ndilo ambalo tumelikopa kutoka kwa wenzetu Zanzibar, Kiingereza cha amali ni ‘Vocation’ kwa hiyo tunatumia amali ili hata yule mtu ukimuita fundi kumbe yeye ni msusi anakwambia kwamba mimi sio fundi mimi ni msusi. Lakini amali ni fani inayokufundisha ujuzi wa kutenda. Kabla ya mapendekezo ya kamati kulikuwepo na maneno mengi kuhusu lugha ya kufundishia, mapendekezo yenu yalikuwaje? Maoni yote yametoka kwa wananchi, ukiangalia maoni ya wengi zaidi ya asilimia 50 walipendekeza Kiswahili kuiendelee kufundisha kama lugha ya kufundishia katika shule za msingi na zaidi ya asilimia 70 walipendekeza zitumike lugha zote Kiswahili na Kiingereza katika elimu ya sekondari na ya juu. Hata hivyo, kamati imegundua kwamba kuna madhaifu katika namna ya ufundishaji wa lugha zote Kiswahili na Kiingereza na hii kelele yote ya lugha ya kufundishia nadhani inatokana na hayo madhaifu. Kwa hiyo katika sera na mitalaa tume imependekeza namna lugha zinavyofundishwa ubadilike ili wanafunzi wajifunze matumizi ya lugha yenyewe, waweze kuitumia kujifunza na kuwasiliana. Katika kugundua hilo kwanza tumebadilisha kabisa Kiingereza kitaanza kufundishwa kuanzia darasa la awali, kwa hiyo wanafunzi watakuwa wanasoma miaka sita Kiingereza kabla hawajaanza kukitumia kama lugha ya kufundishia isipokuwa yale masomo kama historia ya tanzania. Lakini, kuna tofauti kidogo tumesema ili kukidhi matakwa ya lugha zote Kiswahili kianze kutumika kuanzia darasa la kwanza. Ingawa lugha ya kufundishia shule ya msingi ni Kiswahili shule inayotaka kufundisha kwa Kiingereza iombe itaruhusiwa vivyo hivyo hata kwa shule za Sekondari na vyuo zinazotaka kufundisha kwa Kiswahili. Mmeweka utaratibu gani wa maombi na wanafunzi hao watapimwa kwa lugha gani? Kila mwanafunzi atapimwa kwa lugha iliyotumika kujifunzia kama ilivyo sasa hivi shule maalum za Kiingereza zina mtihani wake wa Kiingereza. Ndiyo maana lazima uombe ili vifaa vya kufundishia viandaliwe, mazingira rafiki yaandaliwe. Mlikutana na magumu gani wakati wa kazi ya kukusanya maoni? Kwenye elimu kila mtu ana mawazo yake na akiyashikilia mara nyingi hayupo tayari kubalidilika, kwa hiyo tulikuta watu wana hoja zao, hata kama ni Minority. Mnaweza kuwa mpo kwenye meza watu 200 lakini watu 170 wana mawazo haya lakini ninyi 30 mnamawazo tofauti sasa inafika mahali unajaribu kushawishi unapokea unachakata tu, kwa sababu kazi hii sio tu maoni ni kwamba unachanganya maoni ya wadau, utaalamu na uzoefu, unaangalia hali yetu halisi kwa sababu kuna kitu kinaweza kuwa kizuri lakini katika mazingira yetu kikawa hakitekelezeki. Si kwamba kilikuwa kitu kikubwa sana lakini ilikuwa na changamoto zake, kulikuwa na wadau waliotaka vitu fulani vihusishwe kwenye mtalaa, lakini wakati mwingine ukiujaza sana hautaendana na muda wa kufundishia na unawachosha wanafunzi. Kwa hiyo ilikuwa ni namna ya kuingiza katika mtalaa mambo muhimu bila kuongeza idadi ya masomo na hili tuliliweza kwa kutumia kitu kinaitwa kuchopeka. Kwa mfano unataka tufundishe kuhusu athari za rushwa huwezi kuanzisha somo jipya lakini tunafundisha vitu vingi sana, historia, lugha mbalimbali, sasa unaweza maudhui hayo kuhusu athari za rushwa wakati unafundisha somo fulani. Nini kimewafurahisha zaidi? Kilichonifurahisha zaidi ni mapokeo ya jamii, ilipokea vizuri. Lakini kikubwa zaidi ni kwamba yakitekelezwa tunabadilisha mtindo wa kuwa na vijana waliomaliza shule na kuwa na ujuzi. Kila mwanafunzi atakayetoka katika taasisi ya elimu atakuwa na ujuzi fulani utakaomwezesha kumudu maisha yake. Kipi anajutia? Hapana, unaweza ukachoka lakini sisi watu wa rika letu wakati naenda kidato cha mwaka ilikuwa mwaka 1981 wakati naingia kwenye ukuta nilikuta bango lililoandikwa moja ya hotuba ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Maudhui yake yalikuwa wale wote mnaopata bahati ya kuelimishwa kwa fedha za umma mna deni la kulipa kwa hiyo kazi ilikuwa ngumu ilichukua muda mrefu sana, mimi nilikuwa naona kwamba nalipa kwa jamii iliyoniwezesha kufika hapa. Tunafanya kitu kizuri lakini tunalipa fadhila ya umma kutufikisha hapa. Huyu ndiye Profesa Maboko Profesa Maboko alizaliwa Kibondo mkoani Kigoma na ndiko alikopata elimu ya msingi na Sekondari. Baada ya kuhitimu ngazi hiyo alikwenda Kibaha kwa ajili ya elimu ya kidato cha tano na sita. Alipohitimu, alijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria katika kambi za Makutopora na Nachingwea. Baadaye alikwenda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kwa ajili ya shahada ya kwanza ya Jiolojia na alipohitimu aliendelea kubaki hapo akiwa Mkufunzi mwanafunzi wa Jiolojia. Maisha yake ya ajira yalianzia chuoni hapo hadi kustaafu, kwa mujibu wa maelezo yake ameitumikia taasisi hiyo ya umma kwa zaidi ya miaka 30. Akiwa mkufunzi chuoni hapo, Profesa Maboko aliendelea na elimu na kuhitimu shahada ya uzamili kisha baadaye alipelekwa nje ya nchi na chuo hicho kwa ajili ya msomo ya shahada ya uzamivu. Kulingana na msomi huyo wa Jiolojia, yeye ni baba watoto na babu wa wajukuu kadhaa.
Serikali imesema itawawezesha wafugaji wadogo kupata pembejeo zinazohitajika ili kuboresha mnyororo
Serikali imesema itawawezesha wafugaji wadogo kupata pembejeo zinazohitajika ili kuboresha mnyororo wa thamani wa shughuli hiyo. Hatua hiyo inatarajiwa kufanyika kupitia mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) unaotekelezwa na Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo nchini. Kutokana na hatua hiyo, uzalishaji wa kuku unatarajiwa kufikia milioni 97. Hayo yalielezwa jijini Arusha jana na Waziri wa Mifugo, Abdallah Ulega alipokuwa anafungua kiwanda kipya cha kutotolea vifaranga chenye thamani ya Dola 3.6 milioni za Marekani (zaidi ya Sh8.83 bilioni). Ulega alisema licha ya kuku kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani katika sekta ya mifugo, kwa muda mrefu haukupata uangalizi wa unaostahili. "Familia nyingi nchini hazifugi kuku pekee bali zinaishi na kuku hazilengi kufuga kwa kujinufaisha kiuchumi,” alisema. Kwa mujibu wa Ulega, asilimia 53 ya kaya nchini zinafuga kuku ambao ni asilimia 18 ya nyama inayoliwa nchini. "Sekta ya kuku sio sekta ndogo kama baadhi ya watu wanavyofikiri. Tutaibadilisha ili iwe na tija zaidi," alisema. Hata hivyo, alisema Serikali itarahisisha usajili wa vifaranga kwa wawekezaji walio tayari. "Hatutakubali uanguaji wa vifaranga vidogo vidogo lakini wakati huo huo hatutakatisha tamaa wawekezaji," alieleza. Alisema Serikali haina mpango wa kupiga marufuku uagizaji wa vifaranga kutokana na kuongezeka kwa mahitaji dhidi ya uzalishaji wa ndani. "Tutaendelea kuruhusu uingizaji wa vifaranga kwa kuwa uzalishaji wa ndani hautoshelezi mahitaji,” alisisitiza. Kuhusu kituo hicho, alisema ni miongoni mwa nyenzo muhimu katika kupunguza uagizaji wa vifaranga nje ya nchi. "Itakuwaje tukipiga marufuku kuingizwa nchini kwa vifaranga?. Itabidi wafunge biashara na itakuwa pigo kwa uchumi,” alisema. Hata hivyo, alisisitiza marufuku ya kuingiza vifaraka kutoka nje ya nchi, iliwahi kusababisha mgogoro kati ya Serikali na wazalishaji wa ndani. "Waagizaji kutoka nje wamekuwa nadhifu siku zote. Walitafuta njia mbadala za kuingiza vifaranga. Wakati fulani hii ilisababisha kuhatarisha ubora wa kuku wanaohitajika. "Tutakuwa makini katika udhibiti wa ubora wa masuala kama hifadhi wakati wa kusajili vifaranga," alifafanua. Katika hatua nyingine, Ulega aliwataka Watanzania kujiandaa kwa ajili ya chanjo kubwa ya magonjwa ya kuku ikiwa ni moja ya hatua za kuleta mabadiliko katika sekta ndogo ya mifugo. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela alisema wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi wanakaribishwa kuanzisha biashara mkoani humo. Alisema Mkoa wa Arusha una faida linganishi katika ufugaji na uwekezaji unaohusiana nao kutokana na uhusiano wake wa kihistoria na uzalishaji katika mifugo. Aliupongeza uongozi wa Kampuni ya Silverlands Tanzania Limited inayomiliki kiwanda hicho, kwa kuamua kuwekeza mkoani humo, akisema kuna ardhi ya kutosha kwa ajili hiyo. Hata hivyo, aliwataka wawekezaji wa sekta ya kilimo na mifugo kuongeza thamani ya mazao yao mapya ili kupata masoko ya uhakika nje ya nchi.
Licha ya Dar es Salaam kuonekana Jiji pendwa na watu, hivi unajua kuwa Pwani ndiyo Mkoa kimbilio la
Licha ya Dar es Salaam kuonekana Jiji pendwa na watu, hivi unajua kuwa Pwani ndiyo Mkoa kimbilio la wengi nchini? Kwa taarifa yako, katika mwaka 2022 jumla ya watu 667,676 walikimbilia Pwani, huku 142,910 wakifungasha virago kulihama Jiji la Dar es Salaam. Kulingana na taarifa ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, idadi ya watu imeongezeka katika Mkoa wa Pwani kutoka milioni 1.35 mwaka 2021 hadi milioni 2.02 mwaka jana. Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 32. Wakati Pwani hali ikiwa hivyo, Dar es Salaam kwenyewe mambo si mazuri, kwani idadi ya watu imepungua kutoka milioni 5.5 mwaka 2021 hadi watu milioni 5.3 mwaka 2022. Hiyo ni sawa na kupungua kwa asilimia 2.6 Kwa muktadha wa kiuchumi, kulingana na wanazuoni wa kada hiyo, ongezeko la watu Pwani lina faida na hasara, kadhalika vivyo hivyo kwa upande wa Dar es Salaam. Kwa mujibu wa wataalamu wa uchumi, gharama kubwa za kupanga vyumba na nyumba ni miongoni mwa sababu zinazowahamisha watu Dar es Salaam, huku kuboreshwa kwa miundombinu na wingi wa fursa ndiyo kunakoifanya Pwani kuwa kimbilio. Wasemavyo wachumi Kuongezeka kwa gharama za maisha katika Jiji la Dar es Salaam ni moja ya sababu inayotajwa kuwahamisha watu kutoka eneo hilo kwenda kwingineko, kama inavyoelezwa na Mhadhiri Msaidizi wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Maria Erasmus. Kulingana na Maria, gharama za malazi katika Jiji la Dar es Salaam ndizo hasa zilizoongezeka maradufu, hali inayowafanya baadhi ya watu kushindwa kumudu maisha. “Bei ya kupanga nyumba au chumba Dar es Salaam ni kubwa mno kwa maisha ya kawaida ni changamoto, watu wanashindwa kuishi kwa sababu hiyo,” alieleza. Kuhusu Pwani, alisema maendeleo ya miundombinu ndiyo sababu ya watu kukimbilia mkoani humo. “Sasa hivi mwendokasi inafika hadi Pwani mtu anaweza kuishi Pwani na akafanya kazi Dar es Salaam na kila siku akafanya safari bila tatizo,” alisema. Ongezeko la fursa za kiuchumi katika Mkoa wa Pwani, ni sababu nyingine inayotajwa na Maria kuchagiza watu kuhamia. “Kuna viwanda vingi kule Pwani kwa hiyo hizo zote ni fursa watu wanahamia eneo kufuata fursa, ukiona wameongezeka ujue na fursa zimeongezeka,” alisema. Hata hivyo, alisema ongezeko la watu katika eneo fulani ni tija kwa kuwa linaongeza shughuli za uzalishaji kutokana na wingi wa nguvu kazi. “Faida nyingine ni kukua kwa shughuli za biashara kwa sababu wanunuzi wanaongezeka kwa hiyo Pwani inafaidika kwa hilo,” alieleza. Mtafiti wa masuala ya uchumi, Thobias Shija alisema ongezeko hilo la watu katika Mkoa wa Pwani, pamoja na faida lakini zipo hasara zake. Panapo watu wengi, alieleza gharama za maisha huongezeka kwa kuwa wafanyabiashara hutumia idadi hiyo kama ongezeko la soko, hivyo bei zitapanda. Akifafanua hilo, Shija alisema ongezeko la gharama za nyumba na vyumba katika Jiji la Dar es Salaam, limechagizwa na idadi kubwa ya watu walioongeza mahitaji. “Kwa hiyo hali kama hiyo inaweza kuukumba Mkoa wa Pwani, kwa kadri watu wanavyoongezeka mahitaji yanaongezeka na wafanyabiashara wanapandisha bei. “Mfano Dodoma kabla ya Serikali kuhamia huko bei ya vyumba na nyumba ilikuwa ndogo lakini sasa ambapo Serikali imehamia huko, nyumba na vyumba vya kupanga vimeongezeka bei,” alisema. Kuhusu kupungua kwa watu jijini Dar es Salaam, Shija alisema kutapunguza gharama za maisha kwa upande mmoja, lakini kutasababisha hasara kwa wafanyabiashara kwa upande mwingine. “Watu wanapopungua masoko yanapungua, wale waliokuwa wanafanya biashara kama za kupangisha nyumba wapangaji watapungua, maana yake watalazimika kushusha bei ili wapate wateja, hiyo itawatia hasara,” alisema. Lakini jambo hilo hilo, alilitaja ni faida kwa wakazi wa Dar es Salaam akifafanua kwa kadri wafanyabiashara watakavyoshusha bei kutokana na kupungua kwa soko na ndivyo wananchi watakavyomudu gharama. “Mfanyabiashara anaumia, mwananchi anafurahia kwa hiyo hii inamuumiza mmoja na mwingine anafurahia,” alieleza. Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila alisema kwa ugeni wake ni vigumu kufafanua lolote. "Kwa ugeni wangu naendelea kujifunza haraka mambo mengi ikiwemo hayo maswali yako," alijibu Chalamila.
Viongozi wa dini nchini wamezuiwa kufanya siasa kupitia majukwaa ya vyama vya siasa, huku wanasiasa
Viongozi wa dini nchini wamezuiwa kufanya siasa kupitia majukwaa ya vyama vya siasa, huku wanasiasa nao wakizuiwa kutumia mimbari za dini kufanya siasa. Zuio hilo, linatokana na kile kilichoelezwa na wadau mbalimbali wa siasa na viongozi wa dini kuwa, hayo yote mbali na kuchochea vurugu, pia ni kinyume na utaratibu wa sheria za nchi. Katazo la viongozi hao wenye ushawishi mbele ya umma, linakuja siku 12 tangu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kiandikiwe barua kwa kuhusisha viongozi wa dini katika mkutano wake. Barua hiyo iliyoandikwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi ililenga kukisihi chama hicho kisitishe mkutano huo, kadhalika viongozi wake walitakiwa kwenda katika ofisi yake siku inayofuata. Chadema ilifanya mkutano huo, Juni 23, mwaka huu kuhusu Mkataba wa Uwekezaji na Uboreshaji Bandari ya Dar es Salaam Kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia DP World. Viongozi wa dini waliokuwepo katika mkutano huo ni Askofu William Mwamalanga na Askofu Maximillian Machumu wa kanisa la Ufufuo na Uzima Kibaha, walioshiriki mazungumzo ya kukosoa mkataba huo. Suala hilo, pamoja na matumizi ya lugha chafu dhidi ya viongozi katika majukwaa ya kisiasa na mavazi ya kijeshi kwa walinzi wa viongozi wa siasa ndiyo yaliyoibua haja ya Jaji Mutungi kuitisha Baraza Kuu Maalum la Vyama vya Siasa. Akizungumza katika baraza hilo, Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Alexander Makulilo alisema ingawa kuna uhusiano kati ya dini na siasa, si ruhusa kiongozi wa dini kushiriki siasa za vyama. "Uhusiano kati ya dini na siasa ni changamani, lakini katika nchi yetu imewekwa sheria ili kuratibu uhusiano huo," alisema. Sheria hizo, alisema zinalenga kuweka mazingira mazuri ya kuleta amani, umoja na mshikamano. Alijumuisha Kwa kufafanua kuwa, "kwa mantiki hiyo sheria zinakataza chama cha siasa kutumia viongozi wa dini kufikia malengo yake ya kisiasa." Si viongozi wa dini pekee, Profesa Makulilo alisema hata watumishi wa umma na vyombo vya ulinzi na usalama haviruhusiwi kushiriki siasa za vyama. Kulingana na msomi huyo, sheria inakataza vyama vya siasa kuwa na vikundi vyovyote vya ulinzi na usalama au mavazi yanayoashiria kijeshi, badala yake Jeshi la Polisi ndilo lililopewa kazi hiyo. Lugha ya matusi ni eneo lingine alilosema vyama vya siasa katika mikutano yake ya hadhara vinapaswa kuziepuka baada ya kutolewa elimu hiyo. "Hii ni kwa sababu sheria inakataza lugha za matusi, kudhalilisha, kutweza utu na kubeza kazi iliyofanywa badala yake inataka kujenga hoja mbadala ndivyo siasa zilivyo," alisema. Alieleza iwapo mazingira hayo yatajengwa na kutekelezwa ipasavyo, Tanzania itafikia maendeleo inayoyatarajia. Awali, akiwasilisha mada Mhadhiri huyo alieleza sababu ya viongozi wa dini kutoruhusiwa kushiriki majukwaa hayo ni hofu ya kusababisha mkanganyiko kwa waumini wao. "Kiongozi wa dini huwa na waumini ambao wamegawanyika kiitikadi za kisiasa, wanapoona kiongozi amezungumza hili inaweza kusababisha vurugu," alisema. Kuhusu lugha za matusi, alieleza sababu ya kuzuiwa kwake ni hatari ya kutokea matumbano baina ya pande mbili. "Leo ukimtusi kiongozi wa chama fulani kwa kuwa anakubalika na ana wafuasi, nao watataka kulipa badala yake watakutukana, mwisho wa hili ni hatari," alieleza. Akifungua baraza hilo, Jaji Mutungi alisema dhamira ya mkutano huo si kumnyooshea kidole yeyote aliyekosea bali ni kuelimishana. "Nimelazimika kusema haya kwa sababu watu huko nje wanasubiri kwa hamu kwamba hili baraza litaisha kweli? Si watatumbuana macho?," alisema. Matamanio yake kilichoazimiwa kitatekelezwa na kila mdau wa siasa kwa maslahi ya siasa safi nchini. Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Joseph Selasini alieleza haja ya wanasiasa kurejea misingi ya nchi ili kuepuka migogoro. "Sisi wakatoriki kawaida viongozi wetu wakizungumza basi ndiyo imeisha hiyo, sasa huyu akipata jukwaani kusema kitu tunachukulia kama maelekezo," alisema. Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Kichungaji kutoka Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Padri Florence Rutaiwa alisema ni jukumu la viongozi wa dini kukemea dhambi inayofanywa na binadamu. Lakini, alisema kiongozi huyo hapaswi kutumia jukwaa la kisiasa kufanya hivyo, badala yake akemee katika membari yake kwa maana msikitini au kanisani. "Ni kweli mwanadamu anayekengeuka lazima akemewe lakini si katika majukwaa ya kisiasa, ni katika mimbari zetu," alisema. Hayo ni kwa sababu, alieleza kiongozi wa dini halengi kuchukua Dola kama ilivyo kwa chama cha siasa. "Hata tunapokwenda kwenye majukwaa ya siasa, kazi yetu ni kuwashauri wafanye siasa za kistaarabu na zinazompendeza Mungu. "Kwa viongozi wa kisiasa wanapotualika watualike kwa ajili ya kuwashauri wafanye siasa za kistaarabu na zile zisizoleta mvurugano na si vinginevyo," alisema. Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Dini ya Kiislamu Tanzania, Sheikh Mussa Kundecha alisema ingawa siasa na dini ni vitu vinavyochangamana utekelezwaji wake ni tofauti. Alisisitiza hoja kuwa ni sahihi kiongozi wa dini kukosoa mabaya yanayofanywa na Kiongozi wa Serikali lakini si kwa kutumia jukwaa la siasa. Jambo lingine alilosema ni matumizi ya jukwaa la kisiasa yanatengeneza mkanganyiko baina ya waumini ambao aghalabu huwa na Itikadi mbalimbali za kisiasa. "Kwa sababu inawezekana anaowaongoza wakawa waumini wa chama fulani cha siasa. Kiongozi wa dini asipande katika jukwaa la kisiasa kuonyesha kwamba chama gani kinafaa na kiongozi gani anafaa," alisema.
Harakati za kupigania ruhusa ya vazi la Hijabu kuvaliwa shuleni na wanafunzi wa dini ya Kiislamu ni
Harakati za kupigania ruhusa ya vazi la Hijabu kuvaliwa shuleni na wanafunzi wa dini ya Kiislamu ni miongoni mwa kumbukumbu zilizoachwa na Sheikh Ally Abasaleh katika kipindi cha uhai wake. Kabla ya miaka ya 1990 vazi hilo halikuruhusiwa kuvaliwa na wanafunzi shuleni, kadhalika lilizuiwa hata katika ofisi mbalimbali zikiwemo za umma. Ingawa vazi hilo lilisharuhusiwa tangu mwaka 1992 na Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi kutotekelezwa kwake kuliibua haja ya kuendelezwa kwa harakati hizo katika miaka inayofuata. Kumbukumbu hizo zinaibuka siku mbili baada ya kifo cha Sheikh Abasaleh kilichotokea juzi, katika Hospitali ya Aga Khan alikokuwa akipatiwa matibabu. Kulingana na waumini wa dini hiyo, kumbukumbu nyingine kuhusu kiongozi huyo wa dini ni harakati alizoziendesha na wenzake kuishinikiza Serikali iruhusu wanafunzi kwenda kuswali Ijumaa. Kabla ya harakati hizo, wadau hao walisema hakukuwa na nafasi ya mwanafunzi wa dini hiyo kupata uhuru wa kuabudu katika siku ya Ijumaa, kwani walipangiwa vipindi vya darasani muda wote. Akizungumza na Mwananchi maziko ya Sheikh Abasaleh, Msemaji wa Shule za Kiislamu nchini, Juma Nchia alisema mafanikio hayo yalisukumwa na juhudi kubwa za kiongozi huyo. Alisema harakati za kudai ruhusa ya vazi hilo shuleni na ofisini, zilianza baada ya uhuru na kufanikiwa miaka 38 baadaye. "Ilianzishwa Shura ya Maimamu na Amiri wa Kwanza alikuwa Sheikh Juma Mbukuzi, siku moja alitangaza kuitaka Serikali iruhusu vazi la Hijabu shuleni na katika ofisi za umma. "Baada ya kutangaza vyombo vya dola vya wakati huo vilimkamata kwa kosa la kufanya uchochezi, aliwekewa mahabusu," alisema. Kutokana na hatua hiyo, alisema Sheikh Abasaleh alihamasisha maandamano ya waislamu kuishinikiza kuachiwa kwa Amiri huyo. Mbali na shinikizo hilo, alisema maandamano hayo yalilenga kudai uhuru wa waislamu kuvaa Hijabu shuleni na katika ofisi za umma. "Yalikuwa maandamano makubwa sana, yaliongozwa na Sheikh Abasaleh akiwa na Sheikh Issa Ponda aliyekuwa Katibu wa Shura ya Maimamu," alisema. Baadaye, Julai 1, 1999 Rais Hayati Benjamin Mkapa wa wakati huo, alitangaza hadharani ruhusa ya vazi hilo kuvaliwa shuleni na kutoa wanafunzi wa Kiislamu kupewa muda wa kwenda kuswali Ijumaa shuleni. Pamoja na hilo, alisema Sheikh Abasaleh aliongoza maandamano ya kushinikiza mabadiliko ya sheria ili kutoa uhuru wa kuabudu. Mwenyekiti wa sasa wa Shura ya Maimamu, Sheikh Issa Ponda alisema kumbukumbu za sheikh huyo ni harakati zake enzi za uhai wake. Alieleza alipokuwa hai akishiriki mabadiliko lukuki yaliyopiganiwa na waislamu kupitia maandamano. "Ni mwalimu mzuri ni mtu aliyekuwa thabiti kuhakikisha haki kwa wote inatekelezwa," alisema Sheikh Ponda. Sheikh Ponda alisema hivi karibuni itatangazwa tarehe ya kufanyika kwa mkutano utakaozungumzia wasifu wa Sheikh Abasaleh. Alieleza kifo cha Sheikh Abasaleh kilitokana na maradhi aliyougua tangu muda mrefu, akianza na ugonjwa wa kutosikia. "Aliugua mara mbili alianza kutosikia, alienda India kwa matibabu akaambiwa hatasikia tena, lakini haya yote yanasababishwa na madhila aliyokutana nayo katika harakati za kupigania dini," alisema. Alisema enzi za uhai wake, Abasaleh aligundua uwepo wa changamoto ya watoto wa kiislamu kukosa elimu ya dini. Kwa sababu hiyo, alieleza Abasaleh aliamua kutembelea shule mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu ya dini. Msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Khamis Mataka alisema kiongozi huyo wa dini ya Kiislamu ni miongoni mwa waliokuwa na misinamo isiyoyumba katika maisha yake. "Hakuwa anatetereka kwenye kusema makosa, anaeleza wazi wazi bila kuogopa, hivi ndivyo alivyokuwa," alisema. Alisema kifo chake, kimeacha kumbukumbu kubwa ya mambo mbalimbali aliyopigania kuhakikisha haki za Watanzania zinafikiwa. Chanzo cha kifo chake Said Abasaleh ni mtoto wa kwanza wa sheikh huyo, alisema baba yake amefariki kwa ugonjwa wa saratani. Alisema ugonjwa aliokuwa nao ulimsababishia uvimbe ambao baadaye ulipasuka na hicho kikawa chanzo cha kufa kwake. "Katika maisha yote na Baba sikuwahi kumuona akikorofishana na mtu, wakati wote alitwambia kusimamia katika maamrisho ya Mungu ndiyo msingi maisha," alisema. Huyu ndiye Sheikh Abasaleh Sheikh Abasaleh alimefariki akiwa na umri wa miaka 76, mbali na umaarufu wake katika dini, pia ni alikuwa Mwalimu katika shule za umma. Amefariki akiwa ameacha watoto nane kutoka kwa wake wawili tofauti na hadi kifo chake ameacha mke mmoja. Mbali na uongozi wake katika dini, Sheikh Abasaleh alikuwa Mwalimu wa masomo ya Kemia, Baolojia na Fizikia.
Ukichukua fomu ya kugombea nafasi ya kisiasa na kwa makusudi ukaacha kuirejesha ili kutoa nafasi kwa
Ukichukua fomu ya kugombea nafasi ya kisiasa na kwa makusudi ukaacha kuirejesha ili kutoa nafasi kwa mgombea mwenzako kupita bila kupingwa, upo hatarini kuzuiwa kugombea kwa miaka 20. Si aliyeacha nafasi pekee, hata kama kwa makusudi umeamua kutorudisha fomu utakumbana na msukosuko wa uchunguzi mkali wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) au Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ili kubaini iwapo uamuzi wako huo umeshinikizwa na rushwa. Hayo ni kulingana na mapendekezo ya Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NaCONGO), kuhusu marekebisho ya sheria tano ambazo ni Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Sheria ya gharama za uchaguzi, sheria ya vyama vya siasa na sheria ya elimu ya uraia. Sheria nyingine waliyopendekeza iboreshwe ni ile ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge, Madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji. Mapendekezo ya NaCONGO kuhusu maboresho ya sheria hizo, ni muitikio wa barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi aliyoiandika kwa vyama vya siasa na mashirika hayo, akitoa siku 10 za kupendekeza. Haja ya marekebisho ya sheria hizo, inatokana na malalamiko ya wanasiasa na baadhi ya wananchi kuhusu kutokuwepo kwa haki na uhuru katika chaguzi mbalimbali nchini. Hata hivyo, licha ya hatua ya maboresho ya sheria hizo inayoendelea kufanywa na Jaji Mutungi, bado wapo wanaoeleza matumaini yao ya kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi yatatokana na kuundwa kwa Katiba Mpya. Miongoni mwa maeneo yanayolalamikiwa katika sheria za sasa zinazosimamia uchaguzi ni wagombea kupita bila kupingwa na Rais wa nchi wa awamu husika kupewa mamlaka ya kuteuwa Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Malalamiko mengine ni kuminywa kwa uhuru wa vyama kushirikiana na kuungana, kukosekana kwa ruhusa ya mgombea huru na baadhi ya wagombea kuenguliwa kwa kukosea kujaza fomu. Hayo yalijitokeza katika mapendekezo ya NaCONGO kuhusu maboresho ya sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge, Madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji. Katika sheria hiyo, baraza hilo lilitaka maboresho yafanyika kumzuia kugombea kwa miaka 20 yeyote atakayebainika amekusudia kutorudisha fomu ili kumpa mgombea mwenzake nafasi ya ushindi bila kupingwa. Pia, lilitaka mgombea anayechukua fomu na kwa makusudi akaacha kuirudisha, achunguzwe na NEC na Takukuru kubaini iwapo uamuzi wake huo umesukumwa na rushwa. Lakini, kwa ujumla baraza hilo, lilisema ili kutekeleza malengo ya sheria hiyo ni vema kuondolewa kwa utaratibu wa kupita bila kupingwa na badala yake anayekosa mshindani apigiwe kura na wananchi kupata ridhaa ya kuongoza. “Pia, sheria itamke kuwa mgombea anayefika katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi na kutomkuta atachukuliwa kuwa amewahi muda wa kurejesha fomu n ahata msimamizi akirudi nje ya muda,” lilipendekeza baraza hilo. Mapendekezo mengine katika sheria hiyo ni kuwepo ruhusa ya mtu kugombea nafasi ya kisiasa bila kudhaminiwa na chama cha siasa kwa maana mgombea huru. “Iruhusiwe kuwa mtu yeyote anayetaka kuomba ridhaa ya Watanzania kuweza kuwaongoza aruhusiwe kufanya hivyo ama kwa kudhaminiwa na Chama cha Siasa, Muungano wa Vyama au. “Wadhamini huru wasiowakilisha chama cha siasa ili mradi ni wapiga kura walioandikishwa katika daftari la kudumu la mpiga kura,” walipendekeza. Sheria ya NEC Pamoja na baraza hilo kupendekeza mabadiliko ya jina la mamlaka inayosimamia uchaguzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) hadi kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, pia limetaka muundo wake ubadilike. Kulingana na baraza hilo, muundo huo uwe na wajumbe tisa kwenye eneo la usimamizi wa tume watakaohusika na kusimamia mamlaka hiyo, huku sehemu ya pili ikiwa ni utendaji wa tume. Lakini, lilitaka kusiwepo chombo chochote chenye mamlaka ya kusimamia uchaguzi kama inavyofanywa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), badala yake jukumu hilo iachiwe NEC. Ili kuongeza uhuru na haki kwa tume, NaCONGO ilipendekeza uteuzi wa wajumbe na Mkurugenzi wa NEC ufanywe na kamati itakayoundwa kwa majukumu ya kusajili wajumbe na kupendekeza majina kwa Rais. “Kamati hii itakuwa na majukumu makubwa mawili, kusajili wajumbe wa tume, kupendekeza majina kwa Rais ambapo wataapa mbele ya Rais ndani ya siku 30,” ilieleza. Kwa mujibu wa NaCONGO, Jaji Mkuu wa Tanzania atakuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo huku wa Zanzibar akiwa Makamu Mwenyekiti na Jaji Kiongozi akiwa Katibu. Wajumbe wake watakuwa ni Naibu Mwanasheria Mkuu, Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika na Zanzibar, Rais wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania, Wawakilishi wawili kutoka kundi la Asasi za Kiraia waliyofanya kazi katika eneo la utawala bora kwa zaidi ya miaka 10 na mmoja lazima awe mwanamke. “Mwakilishi kutoka Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu, na uwakilishi huo uzingatie jinsia,” ilieleza taarifa hiyo. Pamoja na yote hayo, baraza hilo lilipendekeza nafasi ya ujumbe wa NEC na Mkurugenzi inapaswa kuombwa kupitia kwa Katibu wa Kamati teule. Lakini, lilitaka ubobevu usipungua miaka 15 katika taaluma ya sheria, ujaji, wakili mwandamizi viwe sehemu ya vigezo vya mtu kuwa Mkurugenzi wa NEC. “Asiwe mtu aliyewahi kujihusisha na siasa za vyama kwa muda wa miaka mitano kabla ya kuomba nafasi hiyo,” ilieleza taarifa hiyo. Sheria ya gharama za uchaguzi Baraza hilo, lilitaka kuondolewa kwa maeneo yanayowatambua Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala na Maofisa Watendaji Kata kuwa wasimamizi wa uchaguzi, badala yake jukumu hilo libaki kwa watumishi wa NEC. Hatua hiyo, kwa mujibu wa NaCONGO itaongeza uhuru na haki kwa tume. Pendekezo kuhusu kupita bila kupingwa lilirejewa katika sheria hiyo, likitaka kuwepo masharti ya wazi na udhibiti wa ugombea bila kupingwa, kadhalikan kuwe na kipengele kinachohitaji kuchunguzwa kwa mgombea aliyepita bila kupingwa ili kupunguza na kuondoa rushwa. “Kuhakikisha udhibiti wa rushwa na takrima kwenye uchaguzi kwa mgongo wa kupita bila kupingwa,” lilieleza baraza hilo. Baraza hilo, lilitaka sheria iweke masharti kwa vyama vya siasa kutenga fedha za kusaidia wanawake kugombea nafasi za ndani ya vyama, kadhalika viwafadhili kampeni za uchaguzi wa kitaifa. Sheria ya vyama vya siasa Katika sheria hii, NaCONGO ilitaka ufafanuzi wa neno shiriki ili kuondoa utata wa vyama vya siasa nchini kushirikiana na vyama rafiki vya nje ya nchi. “Neno “kushiriki” litolewe tafsiri kamili bila kuathiri ushirikiano wa vyama vya siasa vya Tanzania na vyama rafiki nje ya Tanzania kwenye programu mbalimbali za kujengeana uwezo,” ilisema. Baraza hilo, lilitaka vyama vya siasa vipewe wajibu wa kutunga sera kali zinazozuia vitendo vya ukatili wa jinsia na kingono na Katiba ziwawajibishe wanaobainika kuhusika navyo, ikiwemo kuwaondoa kwenye nafasi za uongozi. Katika sheria hii, baraza hilo lilitaka maboresho yahusishe kuondolewa kwa ukomo wa ushirikiano na kuungana kwa vyama vya siasa, likisisitiza viruhusiwe kufanya hivyo kila vitakapoona inafaa. Kuhusu utatuzi wa migogoro ya vyama, baraza lilitaka kuundwa kwa chombo kwa ajili ya shughuli hiyo na kiongozwe na Mwenyekiti anayepaswa kuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu na Makamu Mwenyekiti Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu kutoka Zanzibar na wote watateuliwa na Rais. Pamoja nao, NaCHONGO ilitaka kuwepo wajumbe saba na kati yao watatu wanapaswa kuwa wanawake. Lilitaka chombo hicho kishughulike na kusuluhisha mgogoro baina ya mwanachama na chama, chama na Msajili wa Vyama vya Siasa, mgogoro kati ya chama cha siasa, muunganiko wa vyama na washirika wake na umoja wa vyama na wanachama wake. Ingawa kilichopendekezwa ndiyo matakwa nya wadau wengi wa siasa, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Mohammed Bakary alisema kilichofanyika si njia sahihi. Alieleza ili kufanikisha maboresho ya sheria na maoni ya wadau, ilipaswa kwanza uandaliwe muswada kwa ajili ya kupelekwa bungeni. “Huu utaratibu uliotumika si sahihi,” alisema mhadhiri huyo.
Hatua ya Chadema kukaidi barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi iliyotaka kisitis
Hatua ya Chadema kukaidi barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi iliyotaka kisitishe mkutano wake uliojadili uwekezaji bandari, imekiweka katika mitego miwili, ama kiadhibiwe au kielimishwe. Mkutano huo ulifanyika jana, katika Uwanja wa Bulyaga Wilayani Temeke, ukilenga kuzungumzia mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uboreshaji bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai. Kadhalika, mkutano huo ulihusisha wadau mbalimbali wakiwemo wanasheria, viongozi a Chadema, viongozi wastaafu wa Serikali na viongozi wa dini. Viongozi wa dini waliokuwepo ni Askofu William Mwamalanga na Askofu Maximillian Machumu wa kanisa la Ufufuo na Uzima Kibaha. Hata hivyo, si hao pekee waliopaswa kushiriki viongozi wengine wa dini walialikwa lakini hawakuhudhuria na kwa mujibu wa Askofu Mwamalanga kutoshiriki kwao kulitokana na kutishiwa. Msingi wa barua ya Jaji Mutungi ni mkutano huo kuhusisha viongozi wa dini ilhali ni jukwaa la kisiasa jambo alilosema ni kinyume na utaratibu stahiki. Hata hivyo, mjadala uliozuka katika mitandao ya kijamii umejikita kwenye hoja kwamba, iweje Chadema iandikiwe barua ya kusitisha mkutano kwa sababu ya kushirikisha viongozi wa dini, ilhali vyama vingine vinafanya hivyo bila kuzuiwa na ushahidi wa picha ulitumwa. Miongoni mwa picha zilizosambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ni ile inayomwonyesha aliyekuwa Sheikh wa Mkoa a Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akishiriki jukwaa la siasa katika mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Akizungumza na Mwananchi jana, Jaji Mutungi alisema kwa nafasi yake anaweza ama kuchukua hatua kama msimamizi wa sheria au kutumia fursa hiyo kukielimisha Chadema na vyama vyote vya siasa kuhusu hilo. Uwezekano huo umetokana na kile alichoeleza kuwa, yeye ni msimamizi wa sheria ya vyama vya siasa, kadhalika ndiye mlinzi wa vyama hivyo. "Haya sio mapambano na hata watu wa dini wana nafasi zao za kikatiba za kushiriki kwenye masuala ya siasa, lakini tutawawekea utaratibu wao," alieleza. Kuhusu hatua ya Chadema kukaidi wito wake na maelekezo ya kusitisha mkutano, Jaji Mutungi alisema pengine hatua hiyo imetokana na ama chama hicho kutoelewa au kimekaidi ndiyo maana ana nafasi mbili za hatua. "Ilikuwa leo nikutane nao tuzungumze tuelimishane, lakini haikufanyika kwa hiyo pengine wamekaidi lakini kwa upande mwingine pengine hawajaelewa," alisema Jaji Mutungi. Lakini, alifananisha kilichofanywa na Chadema kama mtoto kwa mzazi wake, akifafanua leo atakosea kesho ukimwelimisha atakiri makosa na hatarudia. Kuhusu viongozi wa dini kushiriki mkutano ya vyama vingine bila kudhibitiwa naye, alisema ndiyo maana analenga kutoa elimu kwa vyama vyote vya siasa kuhusu hilo. Lakini, alisisitiza kilichofanywa na Chadema kimehusisha kuwatangaza na ushiriki wako haukuwa kwa ajili ya maombi Bali kutatuliwa majukwaa ya siasa kisiasa. "Utaratibu unaotumika sasa haukubaliki kama tulivyowaambia viongozi wa dini, wasiruhusu membari zao kutumiwa na wanasiasa, vivyo hivyo kwa wanasiasa," alisema. Alieleza kiongozi wa dini anaposimama popote kuzungumza huchukuliwa kuwa analiwakilisha dhehebu lake, ilhali ndani yake kuna waumini wenye itikadi tofauti za kisiasa. Wadau watoa neno Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Hadija Mwenda alisema awali kulikuwepo na ruhusa ya viongozi wa dini kushiriki majukwaa hayo. Alisema ndiyo maana taasisi ya kuchunguza uchaguzi ya UDSM (TEMCO) ilishirikiana na viongozi wa dini katika shughuli hiyo. "Lakini ilipofika mwaka 2020, Serikali ilizuia kushirikisha viongozi wa dini kwenye hilo, kuanzia hapo hawakushirikishwa," alisema. Hatua hiyo, alisema inaibua swali kwamba nini kiliifanya Serikali iruhusu ushiriki wa viongozi wa dini katika siasa kabla ya 2020 na ikaamua kuwazuia baada ya mwaka huo. Lakini, alisema Jaji Mutungi anaweza kujenga hoja kupitia matakwa ya Katiba kwamba Serikali haina dini, lakini hoja nyingine anaweza kuijengea kupitia sheria ya usajili wa taasisi za kidini. "Sheria anayoisimamia ya vyama vya siasa haifanani na Ile ya usajili wa taasisi za kidini kwa hapo anaweza kujenga hoja kwamba hawa waaoshirikishwa si watu ninaowasimamia," alisema. Mhadhiri Msaidizi wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Revocatus Kabobe alisema ni kosa chama chochote kuwaalika viongozi wa dini kwenye mkutano wa kisiasa. Kwa msingi huo, alisema Jaji Mutungi alikuwa sahihi, lakini hilo linapaswa lifanyike kwa chama chochote kitakapokiuka utaratibu huo. "Kushirikisha viongozi wa dini kwenye mikutano ya hadhara ya kisiasa ni kuwagawa watu, kwa sababu kiongozi wa dini anapaswa kuwa katikati ili akitoa neno liume pande zote," alisema. Mwisho. Serikali imewataka Wakuu wa taasisi za umma, kujitathmini iwapo utendaji wao unakidhi malengo ya kuanzishwa kwa taasisi hizo. Kauli hiyo ya Serikali imetokana na kile ilichokifafanuwa kuwa, kumekuwa na taasisi kadhaa za umma ambazo utendaji wake hauridhishi. Hoja kuhusu mwenendo wa utendaji wa baadhi ya taasisi inakuja miezi minne baada ya ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere kuweka wazi hasara inayosabishwa na baadhi ya taasisi hizo. Kutokana na hoja hiyo ya CAG, Rais Samia aliwahi kusema baadhi ya taasisi ikiwemo ya Maendeleo nchini (NDC), imekuwa ikiisababishia Serikali hasara. "Kuna haja ya kufanyika tathmini ya utendaji wa baadhi ya taasisi za umma, zipo ambazo tangu nikiwa mdogo zipo zimekuwa zikipata hasara Tu. "Ifanyike tathmini tujue kama kuna haja ya kuendelea kuwepo au zifutwe," alisema Rais Samia alipokea ripoti ya CAG. Hayo yaliekezwa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene alipohutubia mkutano wa viongozi wa Wakala za Serikali. Katika hotuba yake hiyo, Simbachawene alisema kujitathmini huko kutawawezesha kubuni mbinu za kuboresha maeneo yanayowaangusha. "Ukisubiri kutathminiwa na yakaelezwa makosa yako, ukitoka hadharani kuzungumza utaonekana unajitetea, ni bora ujitathmini mwenyewe," alisema. Hata hivyo, Waziri huyo alisema ripoti ya Msajili wa Hazina kuhusu tathmini ya mashirika ya umma inasuburiwa na itakapotoka itabainisha yanayoisababishia Serikali hasara. "Hapo ndiyo tutaona kama kuna ambayo tunahitaji kuyafuta, au yanayohitaji kuundwa upya, lakini hiyo kwa sasa ni kazi ya Msajili wa Hazina susi tunahusika na masuala ya kisera," alisema. Katika hatua nyingine, Simbachawene alizitaka taasisi hizo kupokea mifumo inayoletwa na Serikali ili kurahisisha ufuatiliaji. Kutokana na mabadiliko yaliyofanywa na Serikali ya kuanzisha tume ya mipango, alisema Wakuu wa taasisi watarajie mabadiliko ya miundo ya taasisi zao. Akiwakilisha wakala za Serikali, Mkuu wa Chuo cha Takwimu nchini, Dk Tumaini Katunzi alisema miongoni mwa changamoto zinazokabili utendaji wao ni mfumo wa ajira. Alisema mfumo huo huajiri taaluma ambazo wakati mwingine ni kinyume na zinazohitajika na wakala hizo. "Bado mfumo wa ajira haukidhi uendeshaji wa wakala kwa maana tuna mahitaji tofauti, zipo zinazotoa huduma na zile zinazofanya biashara, ili ziendeshwe kwa ufanisi zinahitaji aina ya watu watakaofanya kazi kwenye wakala hizo," alisema. Kwa sababu taaluma inayohitajika inajulikana na wakala husika, alisema ni vema wapewe mamlaka ya kuajiri au jukumu hilo likasimiwe kwao. "Sisi ndiyo tunaojua taaluma tunazozihitaji kuna haja ya kupewa nafasi ya kuajiri au kukasimiwa jukumu hilo," alisema. Akijibu hilo, Simbachawene alisema mfumo uliopo unatoa nafasi hiyo. Alisema sektretarieti ya ajira inaajiri kwa kupewa vigezo vya taaluma inayohitajika na wakala za Serikali, haiamui yenyewe kuchagua. "Uchaguzi wa vigezo vya waajiriwa vinatoka kwenu, mnahusishwa hadi kwenye usaili na kila eneo, asilimia 85 ya vigezo vya waajiriwa vinatoka kwenu sasa sioni sababu ya mnachohitaji," alisema. Simbachawene alisema Serikali ilibadilisha utaratibu huo kuondoa changamoto zilizokuwepo, ikiwemo nafasi kutolewa kwa upendeleo. "Hivi leo ukipewa nafasi ya kuajiri wewe ndiyo Mtendaji Mkuu wa taasisi, lazima utatoa upendelea kwa watu fulani. "Fikiria mimi Waziri kwa sasa ndiyo nina wageni wengi kwangu kuliko wakati wowote wanaomba ajira, sasa ndiyo nipewe nafasi ya kuajiri nitaacha kupendelea? Ndiyo maana tulitoka huku," alisema. Maeneo mengine yaliyopendekezwa kuboresha ufanisi wa wakala za Serikali kwa mujibu wa Dk Katunzi ni ukinzaji wa majukumu. Alisema bado baadhi ya wakala na Wizara zinagongana kwa majukumu haijulikani nani atekeleze lipi na aache lipi kwa mwingine. Mapendekezo mengine ni kuangalia namna ya kuzipa motisha na nyongeza ya mishahara, kadhalika kuwezeshwa miundombinu ya kazi. Kuhusu motisha na mishahara, Simbachawene alisema ni muhimu nchi kuwa na mfumo mmoja ili kuleta uwiano kwa wote. "Kila Mkurugenzi anapambania watumishi wa taasisi yake waongezewe mshahara, hivi mmewafikiria walimu na wauguzi huko, wote tuwe kwenye skimu Sawa ili kutoa haki kwa wote," alisema.
Ingawa ndoto ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi hutafsiriwa kama kauli ya kisiasa, upo uwezekano wa
Ingawa ndoto ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi hutafsiriwa kama kauli ya kisiasa, upo uwezekano wa kutimia iwapo mambo kadhaa yatazingatiwa kuelekea utekelezwaji wake. Kiu ya biashara hiyo ya nishati nchini kwenda nchi za jirani, ilianza tangu mwaka 2013, Tanzania ikiwa mikononi mwa uongozi wa Dk Jakaya Kikwete. Julai 17, mwaka huo, aliyekuwa Waziri wa Nishati, Profesa Sospeter Muhongo alitangaza tarajio hilo la Tanzania kuingiza nishati yake ya umeme katika soko la nje ya nchi. Kauli hiyo ilitokana na kile kilichoelezwa na Profesa Muhongo kuwa, kulikuwa na matarajio ya mapinduzi katika uzalishaji wa umeme, baada ya kusainiwa mkataba wa ujenzi wa mradi wa Kinyerezi. Kukamilika kwa mradi huo, kulitarajiwa kuongeza uzalishaji wa umeme na hivyo, Tanzania kuwa na ziada ya Megawati 500 kufikia mwaka 2014. Lakini, kukamilika na kuanza kufanya kazi kwa mradi huo, hakukuifanya ndoto hiyo itimie, bado umeme uliozalishwa wakati huo, ulikidhi sehemu ya mahitaji ya nchi na haukutosheleza kuuzwa nje. Nchi za Kenya, Uganda na Malawi ndizo zilizotajwa kuwa soko la awali la umeme kutoka Tanzania na kwa mujibu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) tayari ujenzi wa njia za kusambaza nishati hiyo katika mataifa hayo ulishaanza. Tumaini la uhai wa ndoto hiyo linatokana na ukweli kwamba, tayari Tanesco imefikia uwezo wa uzalishaji umeme zaidi ya mahitaji ya ndani ya nchi. Kulingana na shirika hilo, Tanzania inazalisha megawati 1,872.05 za umeme, huku mahitaji ya nchi yakiwa ni megawati 1,363.94, hivyo kuna ziada ya megawati 508.11. Si hivyo, matumaini mengine ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi yanatokana na utekelezwaji wa mradi wa uzalishaji umeme wa Julius Nyerere (JHPP) unaotarajiwa kuzalisha megawati 2,115. Mei 30, mwaka huu, Waziri wa Nishati, January Makamba alisema ndoto ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi bado ipo, lakini Serikali inahitaji kujiridhisha na mambo kadhaa kabla ya kutimia. Katika mazungumzo yake na kituo kimoja cha redio nchini, Makamba alisema, “ili kutimiza ndoto ya kuuza umeme nje, kwanza ni lazima umeme wetu uwe umejitosheleza kwa watu wetu wa ndani, pili kujenga ‘inter connector’ ambapo kwa sasa vitu vyote hivyo viwili bado havijakamilika.” Itawezekanaje Uzalishaji wa umeme wa kutosha ni moja ya nyenzo muhimu ya kufanikisha Tanzania kuwa na uwezo wa kuuza nishati hiyo nje ya nchi, kulingana na Profesa Emrod Elisante mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Uwezekano wa hilo, anasema unatokana na kutumika ipasavyo kwa vyanzo mbalimbali vya uzalishaji wa nishati hiyo. “Kuna chanzo cha jua, gesi ingawa tunatumia lakini bado chanzo hiki hakijatumika vya kutosha, tunahitaji kuongeza namna ili kituzalishie zaidi,” anasema. Kwa mujibu wa Profesa Elisante, kwenye eneo la gesi asilia pekee inawezekana kupatikana Megawati 850 kutoka zinazozalishwa sasa. Lakini, anaeleza ni muhimu katika uzalishaji na lengo hilo, kuzingatia ongezeko la mahitaji ya ndani, kwa kuwa kadri siku zinavyokwenda na ndivyo wanaohitaji wanaongezeka. Profesa Elisante anaeleza vipo vyanzo vya umeme ambavyo hadi sasa havijaanza kutumika na vikitumika vitakuwa na tija na kuwezesha nchi kuwa na uwezo wa nishati na hata kuuza nje ya nchi. Anavitaja vyanzo hivyo ni umeme wa mabaki ya mazao na mabaki ya viwandani. “Ili kufikia adhma hii na kwa uhakika hatupaswi kuacha chanzo chochote, tuhakikishe viwanda vinazalisha umeme na mabaki ya mazao,” anasema. Mtaalamu wa uchumi kutoka chuo hicho, Dk Samwel Wangwe anasema uwekezaji katika miradi wezeshi kwa usambazaji umeme nje ya nchi ndiyo msingi wa kutimia kwa ndoto hiyo. Ingawa kuna mashaka ya uwezo wa kiuchumi katika kutekeleza hilo, anasema sekta binafsi na wadau wengine washirikishwe kushirikiana na Serikali kwa kuwa gharama za uwekezaji huo ni kubwa. “Uwekezaji ndiyo kila kitu, hapa kunahitajika ufanyike uwekezaji wa usambazaji wa umeme, lakini pamoja na miradi tuliyonayo tuwekeze katika miradi mingine ili wakati tunauza nje, tusipunguze kile kinachotumika ndani ukizingatia mahitaji huongezeka,” anasema. Kuuza umeme nje ya nchi si sifa pekee zipo faida lukuki ndani yake, kama anavyofafanua Dk Wangwe. Anasema kwa kuuza umeme nje ya nchi, Tanzania itapata fedha za kigeni, itaongeza wawekezaji kwa kuwa na uhakika wa upatikanaji wa umeme. Anaeleza mambo hayo yote matokeo yake ni kuimarika kwa uchumi wa nchi. Anatoa angalizo kuwa, utekelezaji wa hilo usiathiri upatikanaji wa huduma kwa wananchi. “Unaweza ukauza huku ndani wanao wanaumia, tuhakikishe miradi itakayotumika kuuza nje inaongezwa ili ufike wakati tuwe tunauza nje huku tunao wa kutumia ndani bila wasiwasi,” anasema. Mtafiti na Mshauri wa masuala ya uchumi, Thobias Shija anasema biashara hiyo inawezekana kwa Tanzania, lakini ni muhimu kwanza ufanyike uwekezaji wa kutosha. Kama alivyoeleza Makamba, anasema ni muhimu Serikali iwe na uhakika wa kutosheleza mahitaji ya ndani na ziada ndiyo ifanyiwe utaratibu wa kuuzwa. Kuimarika kwa mahusiano baina ya Tanzania na nchi nyingine ni moja ya faida aliyoitaja, huku kuongezeka kwa mapato ikiwa ni faida nyingine. “Faida kubwa ni mapato tutazalisha umeme mwingi na kuweza kusambaza nje na hapo tutaingiza fedha kutokana na biashara hiyo na hata hivyo hatutauza bei sawa na tunayowauzia watu wetu wa ndani,” anasema. Lakini, anasema mapato hayo hayatatumika kwenye uzalishaji umeme pekee, bali uwekezaji kwenye maeneo mengine utafanyika na hivyo Tanzania kufaidika. Ongezeko la ajira ni faida nyingine itakayopatikana, akisema kwa kuwa kutakuwa na miradi mingi ya uzalishaji na usambazaji umeme, ni muhimu kuwepo vijana wa kuisimamia. Kwa mujibu wa Shija, ingawa kuna matumaini ya kufikiwa kwa hilo, bado kuna safari ndefu kwani inahitajika nchi ijitosheleze kwa mahitaji yake na ziada ndiyo iuzwe nje. Mshauri wa masuala ya Mabadiliko ya Nishati Afrika, Silas Olan’g alieleza uwezekano wa kuuza umeme nje ya nchi utatokana na nchi kuzalisha umeme wa ziada na kuwa na uhakika wa vyanzo vyake. Anaeleza iwapo nchi itaingia mkataba inapaswa kuwa na uhakika wa usambazaji bila kukoma, ili kuepuka usumbufu kwa wateja. Baada ya kujitosheleza, anashauri umeme huo unapaswa kuingizwa kwenye gridi ya kukanda ili nchi inayonunua ichukue kutoka humo. “Ili kuuza lazima tuingize kwenye gridi ya kikanda ambayo nchi yenye umeme inaingiza humo unatumika na unalipwa na hata ukipungukiwa unatoa kwenye gridi hiyo na unatumia kisha utailipa nchi yenye ziada hiyo,” anasema.
Umefikia umri wa kuoa? umewahi kwenda kwa wazazi wa mwenza wako kuanza taratibu za kufanikisha hilo?
Umefikia umri wa kuoa? umewahi kwenda kwa wazazi wa mwenza wako kuanza taratibu za kufanikisha hilo? Walikueleza nini? Kipi kilikufurahisha na kipi kilikukera au kukukatisha tamaa? Maswali haya yanaakisi uhalisia wa wanayoyapitia vijana wengi wanapoanza mchakato wa kufunga ndoa, hali inayotajwa kuchagiza uwepo wa ndoa nyingi zisizo rasmi. Kulingana na vijana, masharti ya baadhi ya wazazi wa waolewaji yanaweka mazingira magumu kwa kijana kuoa au kuolewa na aghalabu baadhi yao huishia kuishi na kujenga familia bila ndoa. Hoja hiyo ya vijana inatajwa na wazee wa kimila kuwa inatokana na kumomonyoka kwa maadili kunakowafanya waone michakato na taratibu za ndoa ni gharama. Mikasa ya ndoa Johnson Mandela Mkazi wa Dar es Salaam, anasema ndoa ilimshinda kutokana na wingi wa masharti aliyopewa na wazazi wa mwenza wake. Ingawa wawili hao wanaishi pamoja sasa, anasema hawakuwahi kufunga ndoa kwa kuwa alishindwa kutimiza matakwa ya wakwe zake. "Tulienda kujitambulisha, nikaambiwa nipeleke barua nikapeleka, ikajibiwa baada ya siku kadhaa kwa barua, ndani yake ikaandikwa vigezo navyopaswa kutimiza," anasema. Kulingana na Mandela, ng'ombe wawili mmoja dume mwingine jike, mablanketi manne, mavazi ya babu na bibi, fedha ya walezi ni miongoni mwa vigezo hivyo alivyopaswa kulipa nje na mahari. "Wakaniambia hivyo vyote natakiwa kuvithaminisha kwa fedha isipokuwa mablanketi tu, kwa hiyo nikatakiwa kupeleka Sh2.5 milioni nje ya mahari na mahari nilitajiwa Sh2 milioni kwa hiyo jumla nilitakiwa kuwa na Sh4.5 milioni," anasema. Katika masharti hayo, anafafanua Sh2.5 milioni alitakiwa kuilipa yote kwa pamoja na alipangiwa kufanya hivyo baada ya miezi miwili, huku mahari akitakiwa kulipa angalau asilimia 70 baada ya muda huo. "Kwa kuwa tunaishi na mwenzangu bila wazazi kujua tukasema tujipange mambo yakiwa sawa tutafanya lakini huu ni mwaka wa tano sasa na tuna watoto wawili, kusingekuwa na masharti mengi kiasi hicho ningeshafunga ndoa," anasema. Yaliyomkuta Mandela hayatofautiani sana na Caroline Mihizi anayeishi na mwenza wake mwaka wa tatu sasa, kwani alishindwa kulipa faini ya kumzalisha mtoto kabla ya kumuoa. "Nikipata mimba kabla sijaolewa nikazaa, mwenzangu akasema twende nyumbani tulipofika kwa wazazi wangu, pamoja na masharti mengine mwenzangu alitakiwa kulipa Sh3 milioni kama faini ya kunizalisha bila kunioa. "Wazazi wake walikuja kuomba punguzo la faini wakaambiwa ni matusi kwa hiyo haipungui, kwa kuwa mimi na mwenzangu tunapendana tukaamua kuishi bila kuoana," anasema. Kinachoshangaza, anasema pamoja na wazazi kuweka ugumu wa ndoa hiyo kwa sababu ya faini, sasa hivi wanamtambua mwenza wake kama mkwe wao na wanamshirikisha hata kwenye masuala ya kifamilia. Tofauti na mitazamo ya vijana hao, Muhsin Yassin anasema hakuna gharama kubwa kama kijana umejipanga na umedhamiria kuoa. Anaeleza wakati anafanikisha hilo, alilipa Sh5 milioni masuala ya kimila na mahari. "Haikunisumbua kwa kuwa nilikuwa na dhamira hivyo nilijipanga mapema, nimeoa Pemba huko wengi wanasema kuna gharama lakini ukiwa na dhamira unajipanga unafanikisha," anaeleza. Anasisitiza vijana wengi wanaona masharti ya ndoa magumu kwa kuwa tayari wameshaishi na watarajiwa wao, hivyo hawana tena shauku ya kuona watakutana na nini baada ya kuwaoa. "Wewe umeishi na mwanamke miaka miwili alafu unataka kumuoa ukitajiwa hata Sh50,000 utaona kubwa kwa sababu tayari unamjua hakuna kipya ndani yake, unatamani upweke hata bure," anasema. Dickson Mlai anaeleza hakuna sababu ya kuwekwa masharti kwani, hata usipooa utapata haki za ndoa. "Wazazi wangejiongeza ujue, sawa unanipa masharti mengi lakini hata bila masharti yako mimi naweza kuwa na mwanao, mimi naona bora upunguze masharti ili uepushe kuletewa mjukuu bila mwanao kuolewa," anasema. Anasema hofu ya vijana si mahari, bali ni zile taratibu nyingine za kimila zinazotajwa, wakati mwingine huzidi hata kiwango cha mahari. "Umeniambia mahari Sh2 milioni, unahitajika na vitu vingine thamani yake inazidi Sh2 milioni eti mila, nitakuletea mjukuu tuone kama hutampokea," anasema. Kauli hizo za vijana, zinamuibua Silas Martin mmoja wa wazazi anayesema wingi wa vigezo ni kipimo cha uwezo wa muoaji kama ataweza kumhudumia vema mwenza wake. “Usipoweka kipimo hicho utaruhusu mwanao aolewe na mtu ambaye hata mlo wao wa siku changamoto, sasa kama mtu amemudu kuleta vitu vya kimila inatosha kumpima kuwa atamudu majukumu ya familia yake,” anasema. Anasema baadhi ya makabila vifaa vya kimila ni muhimu kulipwa tena vinapaswa kuanza kabla ya mahari ili kuepuka laana kutoka kwa wazee waliotangulia. Mzazi mwingine, Mwantum Tebweta anasema kama mwanawe amependa hana budi kumrahisishia mazingira ili waowane kuepusha matokeo mengine. “Unamuuliza binti yako kwamba mwenzio unamuoanaje, hali yake kiuchumi kama anamudu majukumu ya familia mwanao atakwambia na sisi waislamu mahari anataja binti. “Kwa hiyo atamtajia mwenzie kiwango anachoona atamudu kuhusu mambo ya kimila tutataja kuendana na uchumi wa mwanaume maana tunalenga kutekeleza sio kukwaza ndoa ni jambo la heri,” anasema. Wazee wa kimila Chifu wa kabila la Wapare, Ruben Muyuku anasema kuporomoka kwa maadili ndiko kunakowafanya vijana waone michakato ya ndoa ni migumu. Vijana wa sasa, anasema wanaamua wenyewe kuhusu ndoa bila kuwashirikisha wazazi, hatimaye wanapopewa taratibu za kimila huziona kama vikwazo. “Unajua sisi zamani wazazi wa pande mbili ndiyo wanakutana wanazungumza hata ikitajwa gharama kubwa kiasi gani na yakawekwa masharti mengi, wanajadiliana wanafikia muafaka. “Kutokana na umri wao wanaelewana ama kulipa kidogo kidogo au kupunguziana hadi kiasi kinachostahili kulingana na uwezo wa muoaji, lakini siku hizi vijana wanakurupuka,” anasema. Kwa mujibu wa Muyuku, kuepukwa kwa michakato na kuzirahisisha ndoa ndiko kunakozifanya zisidumu, akisisitiza umuhimu wa kufuatwa mila na desturi kama ilivyokuwa zamani. Kuhusu kutozwa faini iwapo wawili hao wamepata mtoto kabla ya ndoa, anasema tamaduni hiyo imerithiwa kutoka enzi za wazee na lazima ifuatwe. “Hiyo ni dharau yaani mmejiamria wenyewe mkapata mtoto leo ndiyo mnakuja kwangu, alafu unataka nisiwatwange faini, maadili yameshuka sana siku hizi," anasema. Mwenyekiti wa Machifu Tanzania, Tonisiza Antonia anasema kuna haja ya kufanyika mabadiliko kwa baadhi ya mila na desturi ili ziendane na vizazi vya sasa. Hoja yake hiyo inatokana na kile anachofafanua kuwa, vizazi vya sasa ni tofauti na zamani, hilo linatokana na namna vilivyolelewa na hata maisha vinavyokutana nayo. “Tukilazimisha kufanya kila kitu kama zamani tutajikuta tunaangukia pabaya, kipi bora kati ya uletewe mujukuu bila matarajio na ulegeze mashari ili uletewe mjukuu kwa heshima,” anasema. Anasema mahari ni jambo la msingi katika ndoa, ni wajibu muoaji atozwe lakini kusiwepo vizingiti vingine lukuki vitaharibu mipango ya vijana. “Ukisema ufananishe na zamani, enzi hizo vijana walitafutiwa wachumba, siku hizi umtafutie kijana mchumba atamkataa wanakutana masomoni huko, wakikuheshimu ndiyo wanakuja nyumbani, lakini wengine utakuta wanaamua huko huko walipo unaletewa matokeo,” anaeleza. Anasema vijana wa sasa wanapaswa kusilikizwa na kupewa miongozo na sio kuweka ugumu kwenye utekelezwaji wa masuala yenye heshima ya familia. “Tubadilike kuendana na wakati kuna mambo yasiyo ya lazima, muhimu yapungue, dunia imebadilika sasa. Ili mila ziheshimiwe lazima tuwasikilize vijana,” anasema. Viongozi wa dini Akizungumzia hilo, Imam Mkuu wa Msikiti wa Temeke Mwisho, Alhad Mussa Salum anasema misingi ya dini ya Kiislamu inalitaja suala la ndoa kuwa ibada na kwamba halitakiwi kuwekewa uzito. “Mtume Mohammad, anasea ifanyeni dini kuwa nyepesi ukiweka uzito unakiuka misingi ya dini,” alisema. Kwa mujibu wa Salum, dini hiyo inatamka mahari kuwa jambo muhimu katika ndoa lakini si mambo mengine kama mkaja wa babu na vinginevyo. Ingawa si mbaya kulipa hiyo kama ni hiari kati ya muoaji na muolewaji, anasema jambo hilo hilo litageuka kuwa haramu kiama litafanywa kuwa takwa la lazima. “Mkiamua wenyewe kwa hiari yenu mtozane vitu hivyo kwa ajili ya kuonyeshana upendo au furaha katika familia si jambo baya, lakini ukilazimisha litakuwa jambo haramu, kitu muhimu ni mahari pasi na mahari hakuna ndoa,” anasema. Kulazimishwa na masuala hayo ya kimila, Sheikh Alhad anasema ndiko kunakowajengea hofu vijana ya kuingia kwenye ndoa. Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dk Steven Munga anasema kwa kawaida kanisa haliingilii mambo ya mahari na vitu vingine vya kimila waachiwa wazazi na tamaduni zao. Lakini kwa hali ilivyo, anasema kuna umuhimu wa kanisa kuingilia kwa kutoa elimu kwa jamii kuhusu suala hilo ili kurahisisha ndoa badala ya kukwaza. “Huwa najiuliza kwanini haya mambo ya mila hatuyaoni kwenye maeneo mengine yanajitokea kwenye mahari tu, mimi nadhani ni uroho w mali tu,” anasema. Anasema lazima kanisa lifundishe kuwa ndoa si chanzo cha kipato na ikiwezekana mambo yasiyo ya msingi yaondolewe kurahisisha ufungwaji wake. Kanisa lisipofanya hivyo, anafafanua kuna hatari kwa kizazi cha sasa kuingia katika mambo yanayomchukiza Mungu, ukizingatia kumekuwa na majanga mengi siku hizi. “Mungu hakutoa watoto kuwa msingi wa kipato, hili ni jambo jema turahisishe watu waoane ili tuepuke athari nyingine,” anasema Dk Munga. Mchungaji wa Kanisa la Waadventisti Wasabato, Charles Mjema anasema ipo migongano kati ya mila na dini kwenye suala la kuoa. Anaeleza vigezo vya kidini ni ridhaa ya muoaji na muolewaji, wazazi, taarifa kanisani na mahari na kwamba matakwa mengine ya kimila yanahusu mila. “Sisi kwenye dini kinachotakiwa ni muoaji, anayeolewa na wazazi waridhie, lakini taarifa itolewe kanisani, jambo lingine ni mahari hii ni ile inayotajwa sio vile vingine vya kimila vile vinahusu tamaduni,” alisema. Pamoja na vigezo hivyo kuwatisha vijana wengi kuingia katika ndoa kwa upande mmoja, Mchungaji Mjema analitaka kundi hilo kuacha kulalamika kwa upande mwingine. “Vijana wapunguze kupenda vya bure, hakuna ugumu kama utajipanga wanapaswa wajipange mambo yote yatakuwa sawa,” anasema. Mchungaji Mjema anasimulia alivyowahi kuwa mshenga walitumia saa nane kujadili mahari, lakini waliafikiana. “Wazazi walitaja kiasi cha fedha kilichozidi uwezo wa kijana aliyetaka kuoa, tukajadili wakagoma ikabidi tukubaliane kulipa kidogo kidogo lakini vijana waowaje kwanza, jambo likafanyika,” anasema. Nadin Mwamlani ni mshenga mwingine aliyesema kila kitu kwenye kuoa kitakuwa rahisi kama utashirikisha watu sahihi kwenye michakato yake. “Kuanzia kwenye mshenga huwezi kupeleka mtu asiye na heshima ndiyo maana kuna umuhimu wa kupeleka wazee wenye adabu wanaojua kuzungumza na angalau wawe wanafahamu tamaduni za wanaoolewa. “Hiyo itarahisisha mazungumzo lakini kutakuwa na undugu ndani ya mazungumzo hayo, kila kitu kinajadilika, isipokuwa vijana wa siku hizi anayeoa anaenda kujitambulisha mwenyewe, barua anapeleka mwenyewe na mahari mwenyewe na muoaji bado ni yeye yeye haya ni mambo ya kisasa lazima yatakukwamisha,” alisema. Mwisho. Ingawa ndoto ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi hutafsiriwa kama kauli ya kisiasa, upo uwezekano wa kutimia iwapo mambo kadhaa yatazingatiwa kuelekea utekelezwaji wake. Kiu ya biashara hiyo ya nishati nchini kwenda nchi za jirani, ilianza tangu mwaka 2013, Tanzania ikiwa mikononi mwa uongozi wa Dk Jakaya Kikwete. Julai 17, mwaka huo, aliyekuwa Waziri wa Nishati, Profesa Sospeter Muhongo alitangaza tarajio hilo la Tanzania kuingiza nishati yake ya umeme katika soko la nje ya nchi. Kauli hiyo ilitokana na kile kilichoelezwa na Profesa Muhongo kuwa, kulikuwa na matarajio ya mapinduzi katika uzalishaji wa umeme, baada ya kusainiwa mkataba wa ujenzi wa mradi wa Kinyerezi. Kukamilika kwa mradi huo, kulitarajiwa kuongeza uzalishaji wa umeme na hivyo, Tanzania kuwa na ziada ya Megawati 500 kufikia mwaka 2014. Lakini, kukamilika na kuanza kufanya kazi kwa mradi huo, hakukuifanya ndoto hiyo itimie, bado umeme uliozalishwa wakati huo, ulikidhi sehemu ya mahitaji ya nchi na haukutosheleza kuuzwa nje. Nchi za Kenya, Uganda na Malawi ndizo zilizotajwa kuwa soko la awali la umeme kutoka Tanzania na kwa mujibu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) tayari ujenzi wa njia za kusambaza nishati hiyo katika mataifa hayo ulishaanza. Tumaini la uhai wa ndoto hiyo linatokana na ukweli kwamba, tayari Tanesco imefikia uwezo wa uzalishaji umeme zaidi ya mahitaji ya ndani ya nchi. Kulingana na shirika hilo, Tanzania inazalisha megawati 1,872.05 za umeme, huku mahitaji ya nchi yakiwa ni megawati 1,363.94, hivyo kuna ziada ya megawati 508.11. Si hivyo, matumaini mengine ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi yanatokana na utekelezwaji wa mradi wa uzalishaji umeme wa Julius Nyerere (JHPP) unaotarajiwa kuzalisha megawati 2,115. Mei 30, mwaka huu, Waziri wa Nishati, January Makamba alisema ndoto ya Tanzania kuuza umeme nje ya nchi bado ipo, lakini Serikali inahitaji kujiridhisha na mambo kadhaa kabla ya kutimia. Katika mazungumzo yake na kituo kimoja cha redio nchini, Makamba alisema, “ili kutimiza ndoto ya kuuza umeme nje, kwanza ni lazima umeme wetu uwe umejitosheleza kwa watu wetu wa ndani, pili kujenga ‘inter connector’ ambapo kwa sasa vitu vyote hivyo viwili bado havijakamilika.” Itawezekanaje Uzalishaji wa umeme wa kutosha ni moja ya nyenzo muhimu ya kufanikisha Tanzania kuwa na uwezo wa kuuza nishati hiyo nje ya nchi, kulingana na Profesa Emrod Elisante mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Uwezekano wa hilo, anasema unatokana na kutumika ipasavyo kwa vyanzo mbalimbali vya uzalishaji wa nishati hiyo. “Kuna chanzo cha jua, gesi ingawa tunatumia lakini bado chanzo hiki hakijatumika vya kutosha, tunahitaji kuongeza namna ili kituzalishie zaidi,” anasema. Kwa mujibu wa Profesa Elisante, kwenye eneo la gesi asilia pekee inawezekana kupatikana Megawati 850 kutoka zinazozalishwa sasa. Lakini, anaeleza ni muhimu katika uzalishaji na lengo hilo, kuzingatia ongezeko la mahitaji ya ndani, kwa kuwa kadri siku zinavyokwenda na ndivyo wanaohitaji wanaongezeka. Profesa Elisante anaeleza vipo vyanzo vya umeme ambavyo hadi sasa havijaanza kutumika na vikitumika vitakuwa na tija na kuwezesha nchi kuwa na uwezo wa nishati na hata kuuza nje ya nchi. Anavitaja vyanzo hivyo ni umeme wa mabaki ya mazao na mabaki ya viwandani. “Ili kufikia adhma hii na kwa uhakika hatupaswi kuacha chanzo chochote, tuhakikishe viwanda vinazalisha umeme na mabaki ya mazao,” anasema. Mtaalamu wa uchumi kutoka chuo hicho, Dk Samwel Wangwe anasema uwekezaji katika miradi wezeshi kwa usambazaji umeme nje ya nchi ndiyo msingi wa kutimia kwa ndoto hiyo. Ingawa kuna mashaka ya uwezo wa kiuchumi katika kutekeleza hilo, anasema sekta binafsi na wadau wengine washirikishwe kushirikiana na Serikali kwa kuwa gharama za uwekezaji huo ni kubwa. “Uwekezaji ndiyo kila kitu, hapa kunahitajika ufanyike uwekezaji wa usambazaji wa umeme, lakini pamoja na miradi tuliyonayo tuwekeze katika miradi mingine ili wakati tunauza nje, tusipunguze kile kinachotumika ndani ukizingatia mahitaji huongezeka,” anasema. Kuuza umeme nje ya nchi si sifa pekee zipo faida lukuki ndani yake, kama anavyofafanua Dk Wangwe. Anasema kwa kuuza umeme nje ya nchi, Tanzania itapata fedha za kigeni, itaongeza wawekezaji kwa kuwa na uhakika wa upatikanaji wa umeme. Anaeleza mambo hayo yote matokeo yake ni kuimarika kwa uchumi wa nchi. Anatoa angalizo kuwa, utekelezaji wa hilo usiathiri upatikanaji wa huduma kwa wananchi. “Unaweza ukauza huku ndani wanao wanaumia, tuhakikishe miradi itakayotumika kuuza nje inaongezwa ili ufike wakati tuwe tunauza nje huku tunao wa kutumia ndani bila wasiwasi,” anasema. Mtafiti na Mshauri wa masuala ya uchumi, Thobias Shija anasema biashara hiyo inawezekana kwa Tanzania, lakini ni muhimu kwanza ufanyike uwekezaji wa kutosha. Kama alivyoeleza Makamba, anasema ni muhimu Serikali iwe na uhakika wa kutosheleza mahitaji ya ndani na ziada ndiyo ifanyiwe utaratibu wa kuuzwa. Kuimarika kwa mahusiano baina ya Tanzania na nchi nyingine ni moja ya faida aliyoitaja, huku kuongezeka kwa mapato ikiwa ni faida nyingine. “Faida kubwa ni mapato tutazalisha umeme mwingi na kuweza kusambaza nje na hapo tutaingiza fedha kutokana na biashara hiyo na hata hivyo hatutauza bei sawa na tunayowauzia watu wetu wa ndani,” anasema. Lakini, anasema mapato hayo hayatatumika kwenye uzalishaji umeme pekee, bali uwekezaji kwenye maeneo mengine utafanyika na hivyo Tanzania kufaidika. Ongezeko la ajira ni faida nyingine itakayopatikana, akisema kwa kuwa kutakuwa na miradi mingi ya uzalishaji na usambazaji umeme, ni muhimu kuwepo vijana wa kuisimamia. Kwa mujibu wa Shija, ingawa kuna matumaini ya kufikiwa kwa hilo, bado kuna safari ndefu kwani inahitajika nchi ijitosheleze kwa mahitaji yake na ziada ndiyo iuzwe nje. Mshauri wa masuala ya Mabadiliko ya Nishati Afrika, Silas Olan’g alieleza uwezekano wa kuuza umeme nje ya nchi utatokana na nchi kuzalisha umeme wa ziada na kuwa na uhakika wa vyanzo vyake. Anaeleza iwapo nchi itaingia mkataba inapaswa kuwa na uhakika wa usambazaji bila kukoma, ili kuepuka usumbufu kwa wateja. Baada ya kujitosheleza, anashauri umeme huo unapaswa kuingizwa kwenye gridi ya kukanda ili nchi inayonunua ichukue kutoka humo. “Ili kuuza lazima tuingize kwenye gridi ya kikanda ambayo nchi yenye umeme inaingiza humo unatumika na unalipwa na hata ukipungukiwa unatoa kwenye gridi hiyo na unatumia kisha utailipa nchi yenye ziada hiyo,” anasema.
Uwekezaji katika sekta ya elimu, ufadhili wa taasisi za fedha, kujenga uwezo wa ndani na ushirikishw
Uwekezaji katika sekta ya elimu, ufadhili wa taasisi za fedha, kujenga uwezo wa ndani na ushirikishwaji wa sekta binafsi ni miongoni mwa mapendekezo ya Tanzania katika kuwezesha nchi za Afrika kuwa na rasilimali watu yenye tija. Mapendekezo hayo yanakuja wakati ambao, nchi za Afrika zinatajwa kuwa na hali ngumu ya kufikia lengo la kuwa na rasilimali watu yenye tija kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu. Hali hiyo ndiyo iliyosababisha haja ya Wakuu wa nchi za Afrika kukutana na kujadili ili kutoka na kauli moja juu ya namna ya kutengeneza rasilimali watu yenye tija. Mkutano huo ulioanza jana kwa kukutanisha Mawaziri wa kisekta waliojadili hilo, katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam na utafuatiwa na ule wa Wakuu wa nchi unaofanyika leo. Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo uliohusisha mawaziri wa kisekta Afrika, Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango alisema nchi za Afrika zinakabiliwa na changamoto ya kifedha kufikia lengo tarajiwa. Kwa kutambua changamoto hiyo, alisema kuna haja taasisi za kifedha za kikanda na Afrika, kubuni mbinu za kuzifadhili nchi zake kuhakikisha zinakuwa na maendeleo ya rasilimali watu. “Uwekezaji katika rasilimali watu unachukua muda mrefu na hivyo inahitaji gharama nafuu lakini uvumilivu wa muda mrefu,” alisema Dk Mpango. Pendekezo la lingine, alisema kwa kuwa sekta binafsi ni mnufaika mkubwa wa maendeleo ya rasilimali watu, mkutano huo utumike kutafuta mbinu za kuivutia ili ishirikiane na Serikali katika kufanikisha hilo. Alitaka taasisi za mafunzo katika bara la Afrika ziwe chachu ya kujenga uwezo wa rasilimali watu itakayotumika na kusaidia kuimarisha rasilimali za nchi. “Kwa bahati mbaya Afrika inatumia sehemu kubwa ya fedha zake, kuhakikisha inaagiza ujuzi kutoka nje kwa ajili ya kutumika kutumia utajiri wa rasilimali zetu za ndani,” alisema. Hata hivyo, Dk Mpango alisema ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu imebainisha mazingira magumu zinayopitia nchi za Afrika katika kufikia lengo la maendeleo ya rasilimali watu. Kilichoelezwa na Dk Mpango kinasisitizwa na Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba aliyeeleza haja ya sekta ya elimu kufanywa kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya rasilimali watu. “Kwa kutambua umuhimu wa kuwapa vijana wetu ujuzi wa vitendo, Tunasisitiza sana kuimarisha elimu na mafunzo ya ufundi stadi,” alisema. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolfu Mkenda alisema maendeleo ya rasilimali watu si wingi wa binadamu katika taifa, bali ni kile kilichowekezwa ndani ya watu ili wawe wa tija. “Kwenye haya elimu ni muhimu, afya, lishe na mengine lukuki lakini haya ndiyo muhimu zaidi,” alisema. Lakini, alisema ili kuimarisha sekta ya elimu ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya rasilimali watu ni muhimu kuwekeza zaidi kwenye elimu kuanzia kwa watoto wadogo. Akichangia mjadala huo, Waziri wa Hazina nchini Kenya, Profesa Njuguma Ndung’u alisema kuna haja ya kuwa na lishe bora kwa nchi za Afrika ili kuwa na vijana wenye nguvu na uwezo wa kuwa rasilimali watu yenye tija. Hata hivyo, alieleza kuna udhaifu wa taasisi za elimu katika nchi za Afrika ndiyo sababu wanazalishwa wataalamu wasio na sifa za kutumika kama rasilimali watu. Akizungumzia uwezeshaji wa wanawake katika maendeleo ya rasilimali watu, Waziri wa Jinsia, Watoto na Jamii kutoka Ghana, Lariba Abudu alisema elimu, afya na ujasiriamali ndiyo msingi muhimu katika hilo. “Naweza kuthibitisha kwmaba wanawake wote waliopo humu ni wasomi na wanaendelea kusoma kwa sababu kusoma ni mchakato,” alisema. Katika hilo, alisema unapomuelimisha mtoto unapaswa kumuelimusha na mkubwa na mzee kwa kuwa wote hutegemeana. Alisisitiza umuhimu wa kuifanya elimu ifikiwe na wote bila kujali ulemavu, jinsia na jambo lolote linalotazamwa kama kikwazo cha elimu kwa mtu. “Tunapaswa kuanzisha Tehama kwenye shule zetu, sisi Ghana tuna vyumba maalum vya Tehama kwenye shule zetu nyingi, hii itasaidia kuzalisha watu wa ujuzi mbalimbali,” alisema.
Hatua ya Chadema kukaidi barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi iliyotaka kisitis
Hatua ya Chadema kukaidi barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi iliyotaka kisitishe mkutano wake uliojadili uwekezaji bandari, imekiweka katika mitego miwili, ama kiadhibiwe au kielimishwe. Mkutano huo ulifanyika jana, katika Uwanja wa Bulyaga Wilayani Temeke, ukilenga kuzungumzia mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji na uboreshaji bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai. Kadhalika, mkutano huo ulihusisha wadau mbalimbali wakiwemo wanasheria, viongozi a Chadema, viongozi wastaafu wa Serikali na viongozi wa dini. Viongozi wa dini waliokuwepo ni Askofu William Mwamalanga na Askofu Maximillian Machumu wa kanisa la Ufufuo na Uzima Kibaha. Hata hivyo, si hao pekee waliopaswa kushiriki viongozi wengine wa dini walialikwa lakini hawakuhudhuria na kwa mujibu wa Askofu Mwamalanga kutoshiriki kwao kulitokana na kutishiwa. Msingi wa barua ya Jaji Mutungi ni mkutano huo kuhusisha viongozi wa dini ilhali ni jukwaa la kisiasa jambo alilosema ni kinyume na utaratibu stahiki. Hata hivyo, mjadala uliozuka katika mitandao ya kijamii umejikita kwenye hoja kwamba, iweje Chadema iandikiwe barua ya kusitisha mkutano kwa sababu ya kushirikisha viongozi wa dini, ilhali vyama vingine vinafanya hivyo bila kuzuiwa na ushahidi wa picha ulitumwa. Miongoni mwa picha zilizosambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ni ile inayomwonyesha aliyekuwa Sheikh wa Mkoa a Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akishiriki jukwaa la siasa katika mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Akizungumza na Mwananchi jana, Jaji Mutungi alisema kwa nafasi yake anaweza ama kuchukua hatua kama msimamizi wa sheria au kutumia fursa hiyo kukielimisha Chadema na vyama vyote vya siasa kuhusu hilo. Uwezekano huo umetokana na kile alichoeleza kuwa, yeye ni msimamizi wa sheria ya vyama vya siasa, kadhalika ndiye mlinzi wa vyama hivyo. "Haya sio mapambano na hata watu wa dini wana nafasi zao za kikatiba za kushiriki kwenye masuala ya siasa, lakini tutawawekea utaratibu wao," alieleza. Kuhusu hatua ya Chadema kukaidi wito wake na maelekezo ya kusitisha mkutano, Jaji Mutungi alisema pengine hatua hiyo imetokana na ama chama hicho kutoelewa au kimekaidi ndiyo maana ana nafasi mbili za hatua. "Ilikuwa leo nikutane nao tuzungumze tuelimishane, lakini haikufanyika kwa hiyo pengine wamekaidi lakini kwa upande mwingine pengine hawajaelewa," alisema Jaji Mutungi. Lakini, alifananisha kilichofanywa na Chadema kama mtoto kwa mzazi wake, akifafanua leo atakosea kesho ukimwelimisha atakiri makosa na hatarudia. Kuhusu viongozi wa dini kushiriki mkutano ya vyama vingine bila kudhibitiwa naye, alisema ndiyo maana analenga kutoa elimu kwa vyama vyote vya siasa kuhusu hilo. Lakini, alisisitiza kilichofanywa na Chadema kimehusisha kuwatangaza na ushiriki wako haukuwa kwa ajili ya maombi Bali kutatuliwa majukwaa ya siasa kisiasa. "Utaratibu unaotumika sasa haukubaliki kama tulivyowaambia viongozi wa dini, wasiruhusu membari zao kutumiwa na wanasiasa, vivyo hivyo kwa wanasiasa," alisema. Alieleza kiongozi wa dini anaposimama popote kuzungumza huchukuliwa kuwa analiwakilisha dhehebu lake, ilhali ndani yake kuna waumini wenye itikadi tofauti za kisiasa. Wadau watoa neno Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Hadija Mwenda alisema awali kulikuwepo na ruhusa ya viongozi wa dini kushiriki majukwaa hayo. Alisema ndiyo maana taasisi ya kuchunguza uchaguzi ya UDSM (TEMCO) ilishirikiana na viongozi wa dini katika shughuli hiyo. "Lakini ilipofika mwaka 2020, Serikali ilizuia kushirikisha viongozi wa dini kwenye hilo, kuanzia hapo hawakushirikishwa," alisema. Hatua hiyo, alisema inaibua swali kwamba nini kiliifanya Serikali iruhusu ushiriki wa viongozi wa dini katika siasa kabla ya 2020 na ikaamua kuwazuia baada ya mwaka huo. Lakini, alisema Jaji Mutungi anaweza kujenga hoja kupitia matakwa ya Katiba kwamba Serikali haina dini, lakini hoja nyingine anaweza kuijengea kupitia sheria ya usajili wa taasisi za kidini. "Sheria anayoisimamia ya vyama vya siasa haifanani na Ile ya usajili wa taasisi za kidini kwa hapo anaweza kujenga hoja kwamba hawa waaoshirikishwa si watu ninaowasimamia," alisema. Mhadhiri Msaidizi wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Revocatus Kabobe alisema ni kosa chama chochote kuwaalika viongozi wa dini kwenye mkutano wa kisiasa. Kwa msingi huo, alisema Jaji Mutungi alikuwa sahihi, lakini hilo linapaswa lifanyike kwa chama chochote kitakapokiuka utaratibu huo. "Kushirikisha viongozi wa dini kwenye mikutano ya hadhara ya kisiasa ni kuwagawa watu, kwa sababu kiongozi wa dini anapaswa kuwa katikati ili akitoa neno liume pande zote," alisema. Mwisho. Bado wadau wana mashaka juu ya utekelezwaji wa mapendekezo ya tume ya kuboresha utendaji wa taasisi za haki jinai, licha ya wajumbe wa tume hiyo kuonyesha matumaini ya kutekelezwa. Mashaka ya wadau yanatokana na kile walioeleza kuwa, kwa sehemu kubwa mapendekezo hayo yanakinzana na mfumo wa utawala wa nchi, lakini yanahitaji mabadiliko ya mfumo wa sheria unaogusa Katiba na kuibua haja ya Katiba Mpya. Hoja hiyo ya wadau inakuja ikiwa ni siku mbili baada ya wajumbe wa tume hiyo, kueleza matumaini ya kutekelezwa, huku wakitaja sababu tatu za imani hiyo. Sababu hizo kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo, Ombeni Sefue ni utashi wa kisiasa wa Rais Samia Suluhu Hassan, uwezo wa kiuchumi wa Serikali na maendeleo ya teknolojia yatakayowezesha utekelezaji. Hata hivyo, mashaka ya wadau yanatokana na uzoefu wa tume na kamati mbalimbali zilizowahi kuundwa, ambazo mapendekezo yake yalisalia kabatini. Mwaka 1996, Serikali chini ya Rais Ali Hassan Mwinyi iliunda tume kwa ajili ya kupendekeza namna ya kukabili rushwa. Tume hiyo iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba ilifanya kazi yake na kukabidhi ripoti bila kutekelezwa. Kadhalika, iliwahi kuundwa tume ya marekebisho ya sheria ya kumiliki ardhi, iliyoongozwa na Profesa Issa Shivji. Nayo ilitoa mapendekezo lakini utekelezaji haukuonekana. Walichokisema wadau Pamoja na utashi na nia njema ya utekelezwaji wa mapendekezo hayo, Mhadhiri Msaidizi wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Revocatus Kabobe alisema kuna mashaka ya hilo kufanyika. Mashaka hayo yanatokana na kile alichoeleza kuwa, baadhi ya mapendekezo ya tume hiyo yanakinzana na mfumo wa utawala wa nchi. “Baadhi ya mapendekezo yanakinzana na mfumo wa utawala wa nchi kwa mfano lile la kutaka mabadiliko ya utendaji wa Jeshi la Polisi kutoka kutumia nguvu ‘Police Force’ hadi kutoa huduma ‘Police Service’. “Hii inahitaji kufumua mfumo mzima wa jeshi hilo na hilo ni vigumu kutekelezwa bila kufanya mabadiliko ya Katiba yote,” alisema. Katika mazungumzo yake na Mwananchi jana, Kabobe alieleza kunapaswa kuwe na maboresho ya mfumo wote wa sheria zetu unaohusisha Katiba ili kufanikisha kutekeleza baadhi ya mapendekezo. Akizungumzia hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Haki Taarifa, John Kitoka aliyesema kwa sehemu kubwa mapendekezo yaliyotolewa yanahitaji mabadiliko ya mfumo mzima wa sheria. Kwa sababu hiyo, alieleza mapendekezo hayo yanailazimu Serikali kuendeleza na kuharakisha mchakato wa Katiba Mpya ambayo ndiyo sheria mama. “Mapendekezo mengi hayawezi kutekelezeka bila kubadilisha vifungu vya Katiba, hivyo utekelezwaji wake utahitaji mabadiliko makubwa ya sheria ambayo Katiba ipo ndani yake,” alisema. Pamoja na hilo, Kitoka alisema baadhi ya mapendekezo hayo yanahitaji mabadiliko ya sheria yatakayoipunguzia dola madaraka. “Kwa sababu mara nyingi watawala hawapendi sheria ambazo zinawapunguzia mamlaka, nachelea kusema kwamba mapendekezo hayo yatatekelezwa,” alisema. Tofauti na mitazamo ya Kitoka na Kabobe, kulikuwepo matumaini ya utekelezaji kutoka kwa Mhadhiri wa Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Idd Mandi aliyesema tume zinazoundwa kwa ajili ya masuala ya kisheria nyingi utekelezaji hufanyika. “Kuna ile tume ya Pius Msekwa ilitoa mapendekezo mbalimbali na yalisababisha kutungwa kwa sheria nyingi, pia kuna ile tume ya Mark Bomani, ilipendekeza kuanzishwa kwa Shule ya Sheria na hiyo imeanzishwa. “Changamoto ya utekelezaji ni kwenye tume zinazoanzishwa kushughulikia masuala ya siasa na huko mimi sijui,” alisema. Mkurugenzi wa Jukwaa la Katiba, Bob Wangwe alisema anasita kuamini kwamba mapendekezo yaliyotolewa na tume hiyo yatatekelezwa. “Napata kigugumizi kusadiki kwenye maneno isipokuwa natamani na nitakuwa na amani nikiona kuna utekelezaji, tumekuwa na tume nyingi lakini utekelezaji umekuwa si mzuri au haupo,” alisema Wangwe. Kutokana na uzoefu huo, Wangwe ambaye ni mwana wa Mbunge wa zamani wa Tarime (Chadema) marehemu Chacha Wangwe, alisema atahifadhi pongezi na matumaini yake hadi hapo atakapoona utekelezaji umefanyika.
Kumekuwepo na sintofahamu kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya tume na kamati mbalimbali zinazoundwa
Kumekuwepo na sintofahamu kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya tume na kamati mbalimbali zinazoundwa na viongozi wakuu wa Serikali. Tume na kamati hizo huundwa ili kuchunguza masuala mbalimbali, lakini baada ya kukabidhi taarifa zao kwa viongozi, suala la utekelezaji wa mapendekezo hubaki kuwa kitendawili hivyo kusababisha jamii kukosa imani. Hata hivyo, hilo linaweza kuwa tofauti kwa Tume ya Haki Jinai iliyoindwa na Rais Samia Suluhu Hassan chini ya uenyekiti wa Jaji Mkuu mstaafu, Othman Chande Othman. Hatua hiyo imetokana na kile kilichoelezwa na wajumbe wa tume hiyo kuwa, wana imani kubwa na sababu za msingi zaidi ya tatu kuwa mapendekezo waliyoyatoa yanakwenda kutekelezwa kwa vitendo. Miongoni mwa sababu zilizotolewa wajumbe wa tume hiyo ni dhamira ya dhati na utashi wa kisiasa wa Rais Samia, aliyejipambanua kama msimamizi mkuu wa haki na anayehubiri usawa kwa Watanzania. Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki Jinai, Balozi Ombeni Sefue alisema mbali na dhamira na utashi wa dhati wa Rais Samia, lakini ukuaji wa teknolojia na rasilimali fedha zilizopo ni sababu zingine za mapendekezo hayo kutekelezwa kwa vitendo na kwa haraka. Balozi Sefue ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi wakati wa utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Jakaya Kikwete na baadaye Dk John Magufuli, amesema Rais Samia anataka kuona haki za wananchi zinalindwa na kuwa kipaumbele kwenye utawala wake. “Utashi mkubwa wa kisiasa wa Rais Samia ni miongoni mwa sababu zinazotupa imani kwamba mapendekezo ya tume hii yatakatekelezwa,” alisema. Sababu nyingine inayompa imani ya kutekelezwa kwa mapendekezo hayo ni kuimarika kwa hali ya uchumi wa taifa, akirejea changamoto za utekelezaji wa maoni ya nyingine ilichagizwa na mdororo wa uchumi wa wakati huo. “Utekelezaji unategemea na hali ya uchumi, hali ya uchumi leo ni nzuri kuliko awali, lakini kuna maeneleo ya Tehama kwa hiyo Tehama inawezesha,” alisema. Mambo yaliyobainika Hata hivyo, alisema katika shughuli ya kukusanya maoni ya wananchi, wamebaini mambo lukuki ikiwemo ukiukwaji wa sheria inayowapa Wakuu wa Mikoa na Wilaya mamlaka ya kuweka watu mahabusu kwa saa 48. Akizungumzia hilo, Mjumbe wa tume hiyo Jaji Eliezer Feleshi alisema katika ukusanyaji maoni walibaini uwepo wa Wakuu wa Mikoa na Wilaya waliokiuka sheria ya kuamrisha kuwekwa mtu mahabusu kwa saa 48. Kulingana na Jaji Feleshi, sheria inataka kiongozi anayetekeleza hilo atoe taarifa mahakamani kuhusu alichokifanya na asipofanya hivyo amri yake inatenguka. “Uzuri mimi nimefanya kazi katika maeneo yote hayo, ni nadra kuona Mkuu wa Wilaya au Mkoa kapeleka taarifa hiyo katika mahakama,” alisema Jaji Feleshi ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kwa bahati mbaya, alisema viongozi hao wanapotumia vibaya sheria hiyo na ikitokea aliyewekwa mahabusu ameshitaki, shitaka hilo linaihusu moja kwa moja Serikali na si kiongozi husika. “Kwenye shauri moja la Mary Otaro yeye aliwekwa ndani akakaa siku saba baadaye akaifungulia Serikali kesi na ikaamriwa alipwe Sh10 milioni. “Ndiyo maana tume inasema mamlaka haya sasa ni vizuri yatumike kwa kufuata zile sheria zilizopo bila ulazima huo na pale inapotokea wanapofanya hayo watashitakiwa au kufikishwa mahakamani kwa majina yao (Wakuu wa Wilaya na Mikoa),” alisema. Akizungumzia hilo, Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo, Balozi Sefue alisema malalamiko kuhusu viongozi hao yalitolewa na wananchi wengi. “Niwaambie ukweli kuna mahali mtu kasema bwana Mkuu wa Wilaya anavituwa na mpenzi wangu anakusweka ndani Ijumaa hutoki hadi jumatatu,” alisema. Alisema tume hiyo imetaka iwapo majukumu hayo yatabaki kwa viongozi hao, kuwepo kwa masharti ya kufanya hivyo. “Kama wakibaki nayo na sisi hatuna tatizo wakibaki nayo, lakini wayatekeleze vizuri,” alisema. Utitiri wa majeshi Katika ukusanyaji huo, pia walibaini utitiri wa taasisi zenye sura ya kijeshi kama inavyofafanuliwa na mjumbe wa tume hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu, Balozi Ernest Mangu. Licha ya wingi wake, Balozi Mangu alisema tofauti na Jeshi la Wananchi, taasisi nyingine zinazoonekana kubeba silaha kazi yake ni kusimamia sheria. “Na usimamizi wa sheria siku zote haufanywi kwa mtutu wa bunduki, kwa hiyo zile taasisi nyingine zinazotekeleza jukumu la kipolisi zinapaswa kuzingatia misingi ya kazi ya Polisi,” alisema. Alieleza hata kanuni tisa za polisi zilizotungwa, hakuna hata moja inayoruhusu matumizi ya nguvu na hilo litafanyika iwapo kutakuwa na mazingira yanayolazimisha. “Sasa wewe upo tu unapokea wageni umevaa magwanda sasa si unatisha watu? Maana yake tulichokuwa tunaeleza ni wananchi wanasema mbona hawa wanatutisha, maana ukienda kwenye misingi ya kazi ya polisi ni kutengeneza mazingira mazuri na jamii,” alisema. Msingi wa kuepuka matumizi ya silaha na kutisha wananchi alisema ni kuifanya jamii iwe na mahusiano yatakayowezesha kujitolea katika kutoa taarifa za uhalifu na mambo mengine. “Ili kupunguza matumizi ya nguvu tukasema tuanze kuondoa ile sura ya jeshi katika kazi yote ya usimamizi wa sheria na tulipokuwa tunazungumza na wadau hata wanajeshi walitwambia wenyewe ndiyo wanaotoa mafunzo kwa hawa wa Jeshi Ussu. “Na wanajeshi wenyewe walituambia wao hawajafundishwa kusimamia sheria, wamefundishwa kuuwa adui kwa hiyo hawa wanapokwenda kupata hayo mafunzo maana yake muhalifu wanamuona kama adui yao. “Kwa hiyo hata namna ya kumkatama wanamkamata kama adui wakati mwingine pengine huyo mhalifu hajatenda hilo kosa, kuendelea kuwa na taswira za kijeshi inaleta mahusiano yasiyo mazuri kati ya vyombo vyetu na wananchi,” alisema. Akizungumzia hilo, Balozi Sefue alisema, “wakati tunazunguka kukusanya maoni kuna mtu aliuliza kuna Serikali ngapi, kwa sababu navyojua kila Serikali huwa na Jeshi moja lakini hapa ukiamka hujui utakamatwa na jeshi lipi.” Kwa sababu hiyo, alisema tume imetambua haja ya Serikali kuwa na jeshi moja huku mamlaka nyingine kama ya Wanyamapori na nyinginezo zifanye kazi kwa kufuata miongozo yao lakini si kutekeleza majukumu ya kijeshi. Alieleza madhara ya kuwa na majeshi mengi ni kuongeza gharama kwa Serikali na silaha kuwa mikononi mwa wengi. “Kuhusu wale askari wa misitu, wale wanaopambana na wanyama wanapaswa kuvaa kombati kama kawaida, lakini sio hadi yule ambaye yupo ofisini eti naye avae sare na vyeo kibao,” alisema. Hata hivyo, alisema katika mapendekezo hayo hakuna dhamira ya kupunguza nguvu ya jeshi lolote, lakini kinachopendekezwa ni kuwafanya wale wasio kwenye majukumu ya kijehi si lazima wavae magwanda. Lakini Jaji Feleshi alisema hilo ni suala la kikatiba iliyompa mamlaka Rais kuwa Amiri Jeshi Mkuu na mkuu wa Serikali katika ibara ya 33 na kuendelea.
Tume ya kuboresha utendaji wa taasisi za haki jinai, imesema katika utendaji wake, imebaini baadhi y
Tume ya kuboresha utendaji wa taasisi za haki jinai, imesema katika utendaji wake, imebaini baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya waliotekeleza kinyume na sheria utaratibu wa kuwaweka watu mahabusu kwa saa 48. Kauli ya tume hiyo, inakuja baada ya kukamilisha kazi yake ya kukusanya maoni kutoka kwa wananchi kuhusu maboresho ya mfumo wa haki jinai. Tume hiyo iliyoundwa Julai 22, mwaka jana kutokana na malalamiko ya wananchi kuhusu kutotendewa haki na taasisi za haki jina, imekabidhi ripoti yake kwa Rais Samia Suluhu Hassan Julai 15, mwaka huu. Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa tume hiyo, Jaji Eliezer Feleshi amesema viongozi hao wengi walitekeleza utaratibu huo kinyume na matakwa ya sheria. Amesema utaratibu wa kisheria unamtaka Mkuu wa Mkoa au Wilaya atekeleze wajibu wa kuamrisha kukamatwa kwa mtuhumiwa iwapo ametenda kosa hilo mbele yake. Lakini, tofauti na takwa hilo, katika utekelezaji wa majukumu yao, amebaini uwepo wa baadhi ya viongozi hao wanaotumia wajibu huo kinyume. Amesema kwa kuwa anayefanya jambo hilo ametakiwa kutoa taarifa kwa mahakama, wengi hawafanyi hivyo. “Uzuri mimi nimefanya kazi katika maeneo yote hayo, ni nadra kuona Mkuu wa Wilaya au Mkoa kapeleka taarifa hiyo katika mahakama,” amesema. Amesema kwa mujibu wa sheria, iwapo kiongozi huyo hatapeleka taarifa hiyo kwa mahakama, amri yake itatenguka. Hata hivyo, ameeleza sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20, kuanzia kifungu cha 11 kinaelezea kuhusu kukamata. Kifungu cha 16 cha sheria hiyo, amesema kinaelezea mamlaka ya mtu yeyote kukamata anayetenda uharifu mbele yake bila hata waranti.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amesema upinzani unaoendelea dhidi ya mkat
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amesema upinzani unaoendelea dhidi ya mkataba wa uwekezaji na uboreshaji wa bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai, ni ishara ya kuwepo kwa tija katika uwekezaji huo. Hoja yake hiyo inatokana na kile alichokifafanua kuwa, si kawaida ya adui kuunga mkono jambo jema linalofanywa na mpinzani wake, mara nyingi hupinga mwa mambo mema na hupigia makofi mabaya. Kauli ya Chongo ni mwendelezo wa kujibu mapigo ya wapinzani wa mkataba huo uliopata ridhaa ya bunge Juni 10, mwaka huu. Upinzani dhidi ya mkataba huo, unatokana na kile kinachoelezwa na Watanzania kuwa, baadhi ya vipengele vyake vina athari katika maslahi ya nchi na wananchi kwa ujumla. Ukomo wa mkataba, utaratibu wa usuluhishi wa migogoro baina ya pande mbili iwapo itatokea, kutoshirikishwa wananchi katika uamuzi wa kusainiwa kwa mkataba ni miongoni mwa hoja zinazoibuliwa na baadhi ya wananchi wakipinga mkataba huo. Chongolo alitoa kauli hiyo mkoani Tanga jana, alipohutubia wananchi wa Mkoa huo katika muendelezo ya ziara yake na baadhi ya makada wa chama hicho ya kuelimisha umma kuhusu uwekezaji huo. Akitetea hoja yake, mtendaji mkuu huyo wa CCM alisema, “hata siku moja adui hawezi kukuombea shibe, hata waswahili walitwambia adui yako muombee njaa, sasa sisi hawa jamaa mbona wanataka watushauri eti waseme wanatupenda sana, kweli wanatupenda au wanahangaika kutuombea njaa? “Na sisi kwa sababu tumeshagundua hilo tuwafuate au tunyooshe mguu,” alisema. Hata hivyo, Chongolo alihusisha kinachofanyika na maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/25, akisema Ibara ya 22 imeitaka Serikali kuweka msisitizo kwenye kuijenga sekta binafsi. Si hivyo tu, alisema ibara hiyo pia inasisitiza ushirikishwaji wa sekta binafsi katika uwekezaji ikiwemo kuondoa urasimu na kuboresha utendaji wa bandari. Ibara nyingine inayozungumzia hilo, alisema ni ya 59 inayoahidi kuielekeza Serikali kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya kimkakati, ikiwemo bandari, viwanja vya ndege na bandari. “Ili kufikia azma hiyo miradi itatekelezwa kwa kuimarisha na kuboresha huduma za bandari,” alisema akisoma sehemu ya ibara hiyo. Kulingana na Chongolo, uwekezaji unaotarajiwa kufanyika ni sehemu ya kuongeza mifumo ya kujitegemea na kupunguza upokeaji wa fedha za misaada ambazo aghalabu huwa na masharti lukuki. “Kwa nini tuendelee kuwa watu wa kupiga magoti ya kuwa ombaomba, ilhali tuna uwezo wa kuweka mifumo ya kujitegemea,” alisema. Katika hotuba yake hiyo, Chongolo alihusisha upinzani dhidi ya mkataba huo na ule mwenendo wa wanaopinga maendeleo mbalimbali yanayofanywa na Serikali. “Mwaka 2017 tuliamua kujenga bwawa la Julius Nyerere, wakaja wakasema hili bwawa litachukua eneo kubwa la Selous la Hifadhi, wakaweka maneno mengi, wanasema ili tusiharibu hifadhi hii tusithubutu kujenga bwawa hili. Pamoja na kutekelezwa kwa mradi huo, alieleza bado hifadhi hiyo ipo na kwa sasa imebadilishwa jina na inaitwa Hifadhi ya Mwalimu Nyerere. Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo alisema uwekezaji katika bandari hiyo unahitaji takriban Sh3 trilioni ambayo Serikali isingeweza kuitoa kutokana na kuwepo miradi mingine lukuki inayopaswa kutekelezwa. Kukaribishwa kwa mwekezaji huyo, alisema haimaanishi kwamba Serikali haikuwahi kuwekeza, kwani tayari imeshatumia takriban Sh2 trilioni kugharimia maboresho mbalimbali ya bandari nchini. Mwanasiasa Mkongwe, Stephen Wassira alisema Tanzania ipo tayari kupokea marekebisho ya mkataba huo na kwamba yeyote aliyenayo ayawasilishe yatazingatiwa. Mzizi wa malalamiko dhidi ya mkataba huo, alisema ni matamanio ya urais kutoka kwa walalamikaji kutoka ndani na hata nje ya CCM. Mbunge wa Ukonga jijini Dar es salaam, Jerry Silaa alisema mkataba huo unawalinda wanaendesha shughuli katika eneo la mwekezaji. "Kuna wale wafanyakazi wa bandari ya Dar es Salaam mkataba unasema lazima waendelezwe kitaaluma ili wasiwakwamishe," alisema.
Kauli ya kashfa dhidi ya wananchi ni jambo linalotarajiwa kumuingiza hatiani Juma Homera ambaye ni M
Kauli ya kashfa dhidi ya wananchi ni jambo linalotarajiwa kumuingiza hatiani Juma Homera ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya. Hilo linatokana na kusudio la Wakili Philip Mwakilima la kumshitaki Homera kutokana na kile alichoeleza kuwa, amewakashifu wateja wake watatu kwa kuwaita wezi. Ingawa katika barua yake kwa Homera, wakili huyo hajafafanua mazingira ya tuhuma hizo, anachokusudia ni kwenda kumshitaki kiongozi huyo mahakamani. Akizungumza na gazeti hili, Wakili Mwakilima alisema tayari alishamwandikia Homera barua, akimtaka aombe radhi kupitia vyombo vya habari, jukwaa ambalo ndilo alilolitumia kuwakashifu. Pamoja na kuomba radhi, Mwakilima alimtaka Homera awalipe wateja wake hao Sh200 milioni kama fidia ya kuwakashifu kwa kauli hiyo. Aliwataja wateja wake waliokashifiwa ni Alphonce Lusako, Raphael Ngonde, Emanuel Changula na Anyisile Mwabukusi. “Akishindwa kufanya hivyo ajiandae kutenga ratiba ya kuhudhuria mahakamani kujitetea,” alisema. Alisisitiza iwapo kiongozi huyo atatekeleza masharti hayo watasitisha kusudio la kumpeleka mahakamani. Taarifa za kashifa dhidi ya wateja wake, Wakili Mwakilima alisema alizinukuu kutoka kwenye vyombo vya habari mtandaoni. "Hii ni kesi ya madai ina maana tangu kumuandikia barua ilikuwa iwe ndani ya siku tatu awe ametekeleza vinginevyo ajiandae kwenda mahakamani, huu ni utaratibu wa kawaida kisheria kumalizana nje ya mahakama," alisema. Katika barua iliyoandikwa na wakili huyo, ilieleza kusudio la kumshtaki mahakamani Homera kwa kuwakashfu wateja wake.
Hatimaye matumaini ya kurejea kwa ibada katika Kanisa la Kiinjili la Kulitheri (KKKT) Dayosisi ya Ku
Hatimaye matumaini ya kurejea kwa ibada katika Kanisa la Kiinjili la Kulitheri (KKKT) Dayosisi ya Kusini Mashariki mkoani Mtwara yanaonekana, baada ya kupatikana kwa uongozi mpya wa nyumba hiyo ya ibada ya waumini wa dini ya kikristo. Kupatikana kwa uongozi mpya, kumetokana na uchaguzi uliofanyika Julai 18, mwaka huu uliomchagua Mchungaji Yeriko Ngwema kuwa askofu mteule wa kanisa hilo, huku Mchungaji Geofrey Mposola akiwa msaidizi wake. Uchaguzi huo uliotanguliwa na Mkutano wa Sinodi wa Julai 17, mwaka huu, umefanyika miezi minne baada ya kuisha kwa fukuto la migogoro ndani ya kanisa hilo, lililodumu kwa zaidi ya miaka sita. Mgogoro ndani ya kanisa hilo, uliochagizwa na kutotakiwa kwa Askofu Lucas Mbedule aliyekuwa kiongozi na kwamba umekoma Machi mwaka huu, baada ya Askofu Mkuu wa KKKT, Frederick Shoo kuunda kamati ya watu 11, kuushughulikia. Akizungumza katika misa maalum baada ya uchaguzi huo, Askofu Shoo ambaye pia alishiriki mkutano wa Sinodi, alimtaka Ngwema kuhakikisha kiti cha uaskofu kinarejea ndani ya kanisa kuu ili ibada ziendelee. Kwa mujibu wa Askofu Shoo, kwa muda mrefu kiti cha uaskofu hakikuwa ndani ya kanisa hilo hivyo ni vema kikarudishwa. “Nasisitiza kuwa kuanzia jumapili ijayo hakikisheni kiti cha askofu kinarudi kanisani sameheaneni katika pendo la kristo, naamini askofu mteule na msaididizi, wajumbe wa baraza kuu mmenisikia kwa maono na toba naamini mnanielewa,” alisema. Manung’uniko, alisema si chanzo cha baraka na aliwataka wafuate katiba ya kanisa hilo na kusimamia neon la Mungu. “Hata mlipopita kwenye mawimbi bado hamkuacha kuabudu wapo watu wakiona mawimbi makubwa wanaacha kuabudu asanteni mmelifanya lile Mungu analotaka sameheaneni na msahau yaliyopita,” alisema. Askofu mstaafu wa kanisa hilo, Mbedule alisema kwa kuwa ameshastaafu atakachokifanya ni kuendelea kuwaheshimu viongozi wa kanisa hilo na kwamba hana kinyongo ya yeyote. “Sina kinyongo na washariki wala viongozi, nitaendelea kuwaheshimu kikubwa shirikianeni tumewachagua viongozi wapya nashukuru uchaguzi umeisha salama,” alisema. Alipopewa nafasi ya kuzungumza, Askofu Ngwema aliahidi kuwaunganisha waumini ili kurejesha heshima ya kanisa hilo mkoani Mtwara. ”Nimeupokea wito huu kwa unyenyekevu mkubwa sana kila mwenye mapenzi mema atuombee ilitufanye mapenzi ya mungu iweze kukua na kusonga mbele,” alisema. Mchungaji Mposola alisema hayakuwa matarajio yake kuwa sehemu ya uongozi wa kanisa hilo na kwamba atafanya kazi kuhakikisha anatekelezwa wito huo wa Mungu. “Napenda kuona Mungu akinitumia na akinisaidia kufanya vile ambavyo anapenda kwa sababu katikati ya wengi nimeonekana kwa ajili ya kujenga na kusogeza mbele dayosisi yetu,“ alisema. Erick shumbusho ni katibu na mtunza hazina wa usharika huo, alisema ni imani yao kuwa uchaguzi uliofanyika umewapa kiongozi atakayeendeleza dayosisi hiyo. “Tunafurahi huduma ya kanisa letu imerejea hata amani imerejea kwetu tunafurahia ilikuwa kelele za miaka mingi tunashukuru kupata kiongozi mpya wa kuongoza dayosisi yetu” alisema Shumbusho. Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa tatu wa Sinodi, Francis Mandamo alisema mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe 125 kutoka katika majimbo saba yanayounda Dayosisi hiyo. Aliyataja majimbo hayo ni Magharibi linalojumuisha Usharika wa Masasi, Ndanda na Mtandi, Jimbo la Pwani usharika wa Mtwara Magomeni, jimbo la kaskazini linajumuisha usharika wa Lindi mjini, Ingawali na Nyangao. Mengine ni Jimbo la Kusini linajumuisha usharika Tandahimba na Newala, Jimbo la Kaskazini Magharlibi linajumuisha usharika wa Nachingwea Ruangwa na Liwale, jimbo la Mtambaswala linajumuisha Mtambaswala yenyewe na usharika wa Mangaka na Jimbo la Kilwa linajumuisha usharika wa Kilwa na Somanga.
Rais Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kutokana na kifo cha aliyewahi kuwa Mwenyekiti
Rais Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kutokana na kifo cha aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha. Jecha amefariki dunia leo, Julai 18, 2023 katika Hospitali ya Lugalo alikokuwa akipatiwa matibabu. Kumbukumbu ya wengi kwa Jecha ni tukio alilolifanya Oktoba 29, mwaka 2015 alipotangaza uamuzi wa kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu visiwani Zanzibar. Hatua yake hiyo ilitokana na kile alichoeleza kuwa, uchaguzi huo uligubikwa na kasoro lukuki. Hata hivyo, ilikuwa mara ya kwanza matokeo ya uchaguzi kufutwa visiwani humo. “Kumegundulika kasoro nyingi katika uchaguzi huu miongoni mwa hizo ni kubainika kwa baadhi ya vituo hasa Pemba vimekuwa na kura nyingi kuliko daftari la wapiga kura wa kituo husika," alisema Jecha alipotangaza uamuzi wa kufuta matokeo hayo. Lawama zaidi ziliibuka dhidi yake kutoka kwa wanasiasa kutokana na kilichoaminiwa kuwa, uamuzi wake wa kufuta matokeo ulitokana na anguko la CCM kwenye uchaguzi huo, hivyo isingekuwa rahisi kuipa ushindi CUF iliyodaiwa kushinda. Hatua ya kufutwa matokeo, ilisababisha uchaguzi huo urudiwe Machi 30 ya mwaka uliofuata. Hata hivyo, aliwashangaza wengi pale alipotangaza nia ya kuwania urais kupitia CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, jambo lililoongeza shaka ya wanasiasa kuhusu uadilifu wake katika kipindi cha uenyekiti wa ZEC. Salamu za rambirambi za Rais Samia kutokana na msiba huo, amezituma leo, Julai 18, 2023 kupitia taarifa kwa vyombo vya habari iliyotiwa saini na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus. “Rais Samia amepokea taarifa za kifo cha marehemu Jecha kwa majonzi makubwa na masikitiko makubwa,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo. Mbali na salamu kuhusu msiba wa Jecha, Rais Samia pia ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Rais wa awamu ya tatu, Hayati Benjamin Mkapa, kutokana na kifo cha Bernard Mkapa (kaka wa Hayati Benjamin Mkapa). “Rais Sami8a amewaomba wanafamilia wote wawe na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na anawaombea marehemu wote wapumzike mahali pema peponi, Amina,” imeeleza taarifa hiyo.
Benki ya Uwekezaji barani Ulaya (EIB), inatarajia kutoa Sh1.8 trilioni nchini ili kuongeza uwekezaji
Benki ya Uwekezaji barani Ulaya (EIB), inatarajia kutoa Sh1.8 trilioni nchini ili kuongeza uwekezaji wake katika sekta ya umma na kukopesha benki za biashara, taasisi ndogo za fedha na wajasiriamali. Fedha hiyo inayotarajia kuitoa ni tofauti na Sh454 bilioni ilizotoa kugharimia uwekezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo inayoongozwa na wanawake na ile ya wajasiriamali. EIB inayomilikiwa na nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya imekuwa ikifadhili uwekezaji hasa kwenye maeneo ya miundombinu, teknolojia ya digitali na uvumbuzi, nishati, mabadiliko ya tabianchi na maendeleo ya biashara ndogo na za kati. Matarajio ya ongezeko la uwekezaji huo, yalitangazwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Makamu wa Rais wa EIB, Thomas Ostros alipofanya ziara ya kutembelea Wizara ya Fedha na washirika wake, ikiwemo Benki ya Dunia. Alisema kati ya fedha hizo tayari Sh1.34 trilioni zimeshatolewa na kwamba zilizobaki zinatarajiwa kutolewa wakati miradi hiyo inaanza kutekelezwa. “Fedha hii tunayotoa ni baada ya uwekezaji wa miradi 28 tulioufanya nchini hadi sasa,” alisema. Katika miradi hiyo 28 ambayo EIB imesaidia umo ule wa Mpango wa Majisafi na Usafi wa Mazingira wa Ziwa Victoria mkoani Mwanza 1 na Mradi wa Umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). Mingine ni uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, mtambo wa kufua umeme wa Kihansi na mikopo kwa benki ili kusaidia wafanyabiashara wadogo na wa kati, hasa uchumi wa bluu na miradi inayoongozwa au kumilikiwa na wanawake. Mbali na miradi hiyo, alisema kwa sasa benki hiyo inaandaa miradi mipya kadhaa ukiwemo wa usimamizi wa taka ngumu jijini Tanga. “Nimefurahishwa sana kwamba timu ya EIB kutoka kituo kikuu cha kanda ya Nairobi inafuatilia miradi ambayo tungependa kuunga mkono Serikali katika kuitekeleza. “Mfumo wetu wa biashara unaangalia kuhakikisha tunashirikiana na Serikali katika kufikia malengo ya maendeleo ya pamoja ambayo pia ni vipaumbele vya Serikali vinavyoboresha maisha ya wananchi," alisema. Akizungumzia hilo, Naibu Katibu Mkuu Menejimenti ya Fedha za Umma Tanzania, Amina Shaaban alisema ziara ya taasisi hiyo inafanyika wakati muafaka kwani, Tanzania inahuisha Dira yake ya Maendeleo yam waka 2050. “Tunaikaribisha EIB na mijadala yenye manufaa ambayo tumekuwa nayo kuhusu msaada wao kwa miradi ya maendeleo tunayoweza kushirikiana nao,” alisema. Katika hatua nyingine, Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba ameikaribisha Taasisi ya kifedha ya Uingereza ‘British International Investment’ kufanya uwekezaji nchini katika sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo nishati. Katika majadiliano ya ushirishikiano na ujumbe wa taasisi hiyo jijini hapa, Dk Nchemba aliyataja maeneo muhimu ya uwekezaji katika sekta ya nishati ni usambazaji wa umeme, mafuta na gesi kwa kuwa Tanzania ina akiba kubwa ya hydrocarbon yenye gesi na mafuta. “Maendeleo ya miundombinu hiyo ni kipaumbele kikubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania na inatarajia kuwa na matokeo makubwa na ya haraka katika kuongeza ajira na kukuza kipato,” alisema Dk Nchemba. Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Simon Cheung alieleza utayari wa taasisi hiyo kujadiliana na Tanzania na kuweka kipaumbele cha uwekezaji katika maeneo mbalimbali.
Ziara ya Rais wa Hungary nchini, Katalin Novak inatarajiwa kuwa ukurasa mpya wa kuimarika kwa ushiri
Ziara ya Rais wa Hungary nchini, Katalin Novak inatarajiwa kuwa ukurasa mpya wa kuimarika kwa ushirikiano wa mataifa hayo katika maeneo ya biashara na utalii, ambayo kwa sasa yamedorora. Rais Katalin amewasili nchini Tanzani juzi kwa ziara ya kiserikali anayotarajia kuihitimisha Julai 20, mwaka huu ikiwa ni sehemu ya mpango wa taifa hilo la Ulaya wa ushirikiano wake na Afrika. Ziara ya mkuu huyo wa nchi, inafanyika kipindi ambacho ushirikiano wa Tanzania na Hungary katika biashara na utalii umedorora. Kwa mujibu wa Rais Samia Suluhu Hassan, urari wa biashara kati ya nchi hizo ni Dola za Marekani 4.2 milioni (zaidi ya Sh10.3 bilioni) mwaka 2022, huku idadi ya watalii waliotembelea Tanzania kutoka Hungary mwaka huo ni 7,188. Akizungumza na waandishi wa habari katika ziara hiyo Ikulu ya Dar es Salaam jana, Rais Samia alisema ujio wa mkuu huyo wa nchi ni tumaini jipya la kuongezeka kwa watalii kutoka Hungary watakaotembelea Tanzania. Si watalii pekee, alisema ziara hiyo imefungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika biashara na uwekezaji hivyo ni miongoni mwa sekta zinazotarajiwa kukua. “Ni ukweli kwamba biashara kati ya nchi zetu ni ndogo lakini kuna mwanga wa kuimarisha na katika hili tumekubaliana kuweka mikakati ya kutumia fursa nyingi zaidi,” alisema. Kuhusu mazungumzo yao, alisema wamekubaliana kuimarisha mahusiano kwa kuanzisha maeneo mapya ya ushirikiano kwa maslahi ya nchi zote na wananchi wake. “Tumekubaliana umuhimu wa kuanzisha mashauriano ya kidiplomasia kati ya nchi yetu, hili litawezesha nchi zetu kuingiliana na kuwa na mashauriano muhimu katika maeneo tuliyokubaliana,” alisema. Kulingana na Rais Samia, katika mazungumzo hayo wamekubaliana kuhamasisha wawekezaji kutoka Hungary kuwekeza nchini katika maeneo ya kimkakati. Aliyataja maeneo hayo ni nishati jadidifu, utalii, Tehama, madini, uvuvi, uzalishaji na fedha. Katika sekta ya elimu, Rais Samia alisema Hungary imekuwa mashirika mkubwa wa Tanzania hasa kwenye elimu ya juu. “Kwa pamoja tumeongeza ushirikiano katika sekta hii kupitia program maalumu ya Hungary na leo (jana) tumeshuhudia saini ya makubaliano ya kuimarisha ushirikiano wetu katika elimu,” alisema. Kutokana na makubaliano hayo, alieleza yamekuja na jambo jipya ambalo wanafunzi kutoka Hungary watapata ufadhili wa masomo na kusoma katika vyuo vikuu vya Tanzania na wataanza wanafunzi watano. Alieleza wamekubaliana kuwa suala la usawa na jinsia na uwezeshaji wa wanawake kuwa miongoni mwa vipaumbele muhimu katika ajenda za Serikali zao. Akizungumza katika mkutano huo, Rais Katalin alisema pamoja na mazungumzo kuhusu ushirikiano, amemwalika Rais Samia kwenye mkutano wa viongozi wanawake anaouandaa kufanyika mwakani na ameridhia kushiriki. Mbali na mkutano huo, mkuu huyo wa nchi alisema amemwalika pia Rais Samia kushiriki katika mkutano kuhusu sensa unaoandaliwa kufanyika Septemba mwaka huu nchini Hungary. “Tumezungumza juu ya changamoto tunazozipitia kwa kuwa sisi tunapakana na Ukraine kwa hiyo tumepokea wakimbili milioni mbili na tunakabiliwa na changamoto za kiuchumi zinazotokana na vita vinavyoendelea kati ya Urusi na Ukraine,” alisema. Kuhusu ushirikiano katika ufadhili wa masomo ya wanafunzi kutoka nchi hizo mbili, alisema haitawasaidia kusoma pekee, bali hata kujua tamaduni za mataifa hayo na lugha. Katika hatua nyingine, Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba ameikaribisha Taasisi ya kifedha ya Uingereza ‘British International Investment’ kufanya uwekezaji nchini katika sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo nishati. Katika majadiliano ya ushirishikiano na ujumbe wa taasisi hiyo jijini hapa, Dk Nchemba aliyataja maeneo muhimu ya uwekezaji katika sekta ya nishati ni usambazaji wa umeme, mafuta na gesi kwa kuwa Tanzania ina akiba kubwa ya hydrocarbon yenye gesi na mafuta. “Maendeleo ya miundombinu hiyo ni kipaumbele kikubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania na inatarajia kuwa na matokeo makubwa na ya haraka katika kuongeza ajira na kukuza kipato,” alisema Dk Nchemba. Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Simon Cheung alieleza utayari wa taasisi hiyo kujadiliana na Tanzania na kuweka kipaumbele cha uwekezaji katika maeneo mbalimbali.
Tume ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoiunda kwa ajili ya kutathmini utendaji wa taasisi za haki jina
Tume ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoiunda kwa ajili ya kutathmini utendaji wa taasisi za haki jinai imekabidhi ripoti yake iliyohusisha mapendekezo ya wadau mbalimbali juu ya mwenendo wa mfumo wa haki jinai. Kwa sehemu kubwa kilichopendekezwa ndicho kile ambacho mara nyingi tumekuwa tukikisikia kutoka kwa wadau mbalimbali wakikosoa na kupendekeza kuhusu utendaji wa taasisi za haki jinai. Hii maana yake ni kwamba kwa kiasi kikubwa tume hiyo imekidhi matakwa ya wadau juu ya kile walichokipendekeza kuhusu uboreshwaji wa mifumo ya haki jinai na hilo linathibitishwa na ukimya wa wadau kuhusu mapendekezo hayo. Mara nyingi kumekuwa na ukosoaji mkubwa kila baada ya tume au kamati mbalimbali zinazoundwa na Serikali juu ya kutathmini utendaji wa idara fulani, lakini kwa tume ya haki jinai hilo sijalisikia kwa hilo tuwape kongole. Pamoja na utendaji wa tume hiyo kuakisi matarajio ya wengi kuhusu utendaji wa taasisi za mfumo wa haki jina, lakini utekelezwaji wa kile kilichopendekezwa ni jambo lingine linaloibua wasiwasi. Wasiwasi huo unatokana na uzoefu wa muitikio wa Serikali juu ya maoni na mapendekezo ya kamati au tume mbalimbali inazoziunda kwa ajili ya kurekebisha au kuboresha mwenendo wa jambo fulani. Mara nyingi kinachopendekezwa na uhalisia wa utekelezaji huwa tofauti, jambo linalopunguza matumaini ya wengi juu ya umuhimu wa kuundwa kwa tume au kamati za kushughulikia mambo hayo. Tuachane na tume nyingine zilizowahi kuundwa, tuzungumzie hii ambayo bado ina uhai. Sehemu kubwa ya ilichokipendekeza hakihitaji muda mrefu wa maamuzi wala vikao vitakavyotumia miezi au miaka kadhaa ili kutekeleza. Kwa kiasi kikubwa vilivyopendekezwa vinahitaji utashi wa viongozi madarakani kuamua vianze kutekelezzwa mara moja na hilo halihitaji muda zaidi. Matumaini yangu ni kwamba haya yanayohitaji utashi wa viongozi na kwa sababu wapo, hakuna sababu ya kutumia muda mrefu kuchakata utekelezwaji wake, uamuzi ufanyike mapema ili kuendana na matakwa ya wananchi. Kwa kadri tutakavyotumia muda mchache kutekelezwa maoni na mapendekezo hayo na ndivyo tutakavyoweka mazingira ya kuaminiwa na umma. Kama mnakumbuka zamani zikiundwa tume kushughulikia changamoto za jamii, umma ulikuwa unazisherehekea, lakini sasa zinatazamwa kama kichaka cha kuchelewesha mahitaji ya jamii. Hayo yanaashiria kupungua kwa imani ya umma juu ya ahadi za viongozi kuhusu changamoto zinazowakabili na hayo yanazidi kuongeza hasira ya wananchi dhidi ya Serikali yao. Ili kuendana na matakwa ya umma ni vema Serikali iwe na hatua za haraka dhidi ya mambo yanayowasumbua wananchi n ahata marekebisho yasisubiri michakato yatekelezwe haraka ili kuokoa wananchi. Ni wazi malalamiko dhidi ya changamoto katika mfumo wa haki jinai yamekuwepo tangu muda mrefu, muda wa utekelezaji uwe mfupi ili kupunguza malalamiko ya wananchi. Wapo wanaolalamikia mahabusu kukaa muda mrefu magerezani kabla ya kesi zao kusomwa, yapo na mengine lukuki ikiwemo ubambikizaji kesi, haya yasitumie muda mrefu yatekelezwe haraka. Kwa kadri tunavyochelewa na ndivyo tunavyoweka mazingira magumu ya kuaminika na umma na hatimaye hakuna tutakalozungumza tukaeleweka. Uharaka wa hatua za kutafuta changamoto za jambo, uendane na ule wa kuliboresha ili kuwepo na maana ya tunachokipambania. Naamini zimetumika gharama katika utendaji wa tume iliyoundwa kushughulikia changamoto katika mfumo wa haki jinai, tuone uchungu wa fedha hizo na tuhakikishe tunatekeleza kinachotarajiwa. Lakini kutekelezwa kilichopendekezwa kunaongeza imani hata kwa wajumbe wa tume hiyo iliyoundwa ya kushughulikia mambo hayo. Wenye wajibu wa kuamua utekelezwaji wake, waamue haraka ili kurekebisha kasoro zilizopo, lakini yale yanayohitaji marekebisho ya sheria, michakato ifuatwe haraka kurekebisha. Lakini, kwa sababu hatua ya kutafuta mzizi wa tatizo ilihusiaha taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari, hata wakati wa utekelezwaji Serikali itoe taarifa ya kila kinachofanyika ili wananchi waelewe. Kusiwe na utekelezaji wa siri kwenye mambo yanayohitaji ushirikishwaji wa jamii, Serikali ihakikishe inatoa taarifa ya utekelezaji wa kila hatua na kila pendekezo na ikiwezekana itoe hata ratiba ya utekelezaji. Wananchi wasiachwe wakisubiri utekelezwaji bila kujua lini utaanza, wapewe taarifa ili wawe na uhakika wa lini machozi yao yatafutika.
Kuimarika kwa ushirikiano katika sekta ya elimu na kuibuka kwa maeneo mapya ya uhusiano ikiwemo uwek
Kuimarika kwa ushirikiano katika sekta ya elimu na kuibuka kwa maeneo mapya ya uhusiano ikiwemo uwekezaji na biashara ni miongoni mwa matarajio ya wadau kutokana na ziara ya Rais wa Hungury, Katalin Novák. Rais Katalin aliwasili nchini jana usiku na anatarajia kufanya ziara ya kiserikali hadi Julai 20, mwaka huu ikihusisha mazungumzo na Rais wa Tanzania, Rais Samia Suluhu Hassan na kusaini makubaliano ya ushirikiano katika maeneo ya biashara na kilimo. Hii ni ziara ya kwanza ya mkuu wa nchi ya Hungury kuja Tanzania na anawasili kipindi ambacho ushirikiano hasa katika biashara baina ya nchi hizo umeporomoka. Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax thamani ya miradi ya Hungury nchini Tanzania ni Dola za Marekani 1.79 milioni (Zaidi ya Sh4.4 bilioni). Ujiuo wa mkuu huyo wa nchi wa kwanza mwananchi nchini Hungury linatarajiwa kuwa tumaini jipya ya kufufuka na kuimarika kwa ushirikiano baina ya nchi hizo. Akizungumzia ziara hiyo jana, Mtaalamu wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Timoth Lyanga alisema kuimarika kwa demokrasia ya kimataifa ni miongoni mwa tija zitakazopatikana kutokana na ziara hiyo. Kulingana na Dk Lyanga, Tanzania na Hungury zimekuwa zikishirikiana kwa muda mrefu katika maeneo ya elimu, kwani wanafunzi wengi nchini wanakwenda kusoma katika nchi hiyo. “Ziara ya kiongozi huyo itaongeza maeneo ya ushirikiano kutoka yale ya awali, lakini ziara hiyo pia inaimarisha ushirikiano katika maeneo waliyoshirikiana awali,” alieleza. Kwa sababu Tanzania ina maeneo mengi ya uwekezaji wa sekta mbalimbali, Dk Lyanga alieleza ziara hiyo itatangaza fursa hizo na hatimaye kuvutiwa wafanyabiashara wa nchi hiyo kuja nchini. Akitangaza kuhusu ziara hiyo, Dk Tax alisema Rais Katalin baada ya kuwasili nchini leo atakutana na mwenyeji wake, Rais Samia na kufanya mazungumzo naye ya siri kisha ya kiserikali yatakayofuatiwa na mkutano na waandishi wa habari. Baada ya mkutano huo, kwa mujibu wa Dk Tax Rais huyo wa Hungury Julai 19 atakwenda Arusha kwa ziara binafsi, kisha Julai 20, mwaka huu ataanza safari ya kurudi nchini kwake. “Safari ataifanya kupitia Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro,” alisema Dk Tax. Akiwa nchini Tanzania, Dk Tax alisema yatasainiwa makubaliano ya ushirikiano katika sekta ya kilimo, biashara, elimu na sayansi na teknolojia. Kwa mujibu wa Dk Tax, ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka Tanzania watakaokwenda kusoma nchini Hungury, kadhalika baadhi ya wanafunzi wa nchi hiyo watakuja nchini kwa ajili ya kubadilishana ujuzi. Katika hatua nyingine, Dk Tax alitangaza uwepo wa mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu uwekezaji katika rasilimaliwatu. Mkutano huo, alisema utafanyika Julai 25 na 26 ukihusisha Mawaziri katika sekta za rasilimaliwatu na kisha wakuu wa nchi. Alisema hii ni mara ya kwanza kwa mkutano huo kufanyika Tanzania na Afrika kwa ujumla. Kuimarika kwa amani, alisema ni miongoni mwa sababu za Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo. Sababu nyingine ya Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo, alisema ni hatua ilizochukua katika kuwaendeleza vijana ikiwemo kuimarisha sekta za elimu na afya. "Tanzania iliombwa kuwa mwenyeji wa mkutano na vigezo ni kwamba Tanzania ni moja ya nchi za Afrika ambazo idadi ya watu inakuwa kwa kasi na ina hazina kubwa ya vijana," alisema. Alieleza katika mkutano huo litatokewa azimio la Dar es Salaam linalolenga kutoa muelekeo na msimamo wa nchi za Afrika kuhusu uwekezaji katika rasimaliwatu. Kamishna wa Fedha za Nje kutoka Wizara ya Fedha, Richard Bade alisema hatua ya Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo, ilitokana na kuombwa na Benki ya Dunia. Alizitaja sababu nyingine za Tanzania kuombwa ni ongezeko la idadi ya watu hasa vijana na uwezo wake wa kutumia mtaji wa vijana katika maendeleo.
Rais Samia Suluhu Hassan ametetea ile hatua yake ya kutengua mara kwa mara viongozi mbalimbali wa Se
Rais Samia Suluhu Hassan ametetea ile hatua yake ya kutengua mara kwa mara viongozi mbalimbali wa Serikali, akisema uamuzi huo unafanywa na mamlaka za uteuzi kwa lengo la kulinyoosha taifa. Katika hoja yake hiyo, Mkuu huyo wa nchi amewataka ndugu na jamaa wa viongozi wanaotenguliwa, waache kulalamikia uamuzi wa mamlaka za uteuzi, badala yake wastahimili kinachofanyika. Kauli ya Rais Samia, imetokana na mada iliyotolewa na Sheikh Sayyid Ayzuddin kutoka Kenya, aliyesema mafanikio ya Mtume Mohammad yalitokana na hatua yake ya kuwapa nafasi katika nyanja mbalimbali wale wanaostahili na si rafiki zake. “Mwenyezimungu alimpa uwezo wa kufanya mambo ambayo yakifanywa na asiyekuwa Mtume atafaulu. Aliwaweka katika kila Nyanja wanaostahiki, hakumuweka katika kila Nyanja anayekuwa wake,” alisema. Tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Tanzania, Machi 19, mwaka 2021, Rais Samia ametengua viongozi mbalimbali na mara ya mwisho ni Julai 3, mwaka huu alipomtengua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Athumani na Wilaya ya Kilindi Abel Busalama. Kauli ya utetezi kuhusu uamuzi wa utenguzi aliitoa visiwani Zanzibar jana, alipohutubia katika Kongamano la Wanawake wa Kiislam kuelekea maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Kiislamu 1445 Hijiria. Alieleza kinachoangaliwa katika uteuzi na utenguzi ni kiongozi atakayefanya vizuri na asiyefanya, lakini kumekuwa na kelele nyingi wanapowaondoa wasiofanya vema. “Tustahimili kuumia kwa mwanao kuondoka, mdogo wako kuondoshwa tustahimili kuumia ili taifa linyooke, vinginevyo tunyooshane tangu nyumbani ili anayepewa dhamana asiwe na mkono mkono. “Asifanye uzembe akaacha kazi akatoka akaenda vijiweni, sisi wakubwa huwa hatustahimili hayo, tuna mambo makubwa tumetoa ahadi ndani na kimataifa, tunataka wasaidizi wetu hawa watusaidie,” alisema. Alieleza anapoonekana mwenye uwezo wa kufanya vema kuliko aliyepo, mamlaka za uteuzi hufanya hivyo na hiyo isichukuliwe kuwa ni upendeleo. “Ndugu zangu hebu tuzipunguzeni zile, kawekwa yule tu, kachukua watu wa huko tu, unamuona huyo kawatoa hawa, kafanya hivi, kafika tu kawaondosha watu wote kafanyaje, mmh,” alisema. Katika hatua nyingine, Rais Samia aliwataka wanawake kujitathmini kwa kuangalia uwezo wao katika mapambano dhidi ya changamoto ya mmomonyoko wa maadili. Ili kufanikiwa kwenye mapambano hayo, aliwataka kwanza kujua ilipo nguvu yao, udhaifu wao na hayo wayafanye wakiwa wenyewe. “Katika kurekebisha maadili yaliyomomonyoka, tuangalie fursa zetu ni zipi, tunaweza kufanya nini, fursa ya kwanza walimu wazuri tunao, Serikali inatuunga mkono, wengi wanajitokeza kutoa mihadhara kuwawezesha wengine,” alisema. Baada ya kuangalia fursa, alisema eneo lingine wanalopaswa kujua ni vikwazo vya kuyafikia hayo wanayoyatarajia. “Unakuta wifi yako ana kazi nzuri anatoka anakwenda kufanya kazi, unakwenda kwake uipomkuta unasema mwanamke gani hatulii nyumbani, hivi ndivyo vikwazo vyenyewe,” alisema. Baada ya kuangalia hatua zote, Rais Samia alisema wanapaswa kurudi kwa Serikali kuieleza eneo wanaloweza kufanya ili kurekebisha mmomonyoko wa maadili. Hata hivyo, mkuu huyo wa nchi alitaka Watanzania kulinda amani, akisema ndiyo msingi wa maendeleo na uchumi wa taifa lolote duniani. “Juzi nilikuwa namsikiliza Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji akawa anaeleza Mei na Juni ndiyo miezi aliyopokea miradi mingi ya uwekezaji, ametaja na gharama zake. “Lakini hayo yametokea kwa sababu kwa jirani panawaka moto, sisi kwetu kuna amani, mwekezaji hawezi kwenda eneo akiambiwa kuna fujo,” alisema. Katika kudumisha amani, alisema ni vema watu wanapokwazana kufikia hatua ya kusuluhisha, badala ya kuishia kukwazana na hatimaye kuhatarisha amani. Akizungumza katika kongamano hilo, Sheikh Ayzuddin alimuomba Rais Samia kutuma tume maalum kwa ajili ya kukwamua vikwazo vya usafiri katika mpaka wa Horohoro na Lungalunga kutoka Kenya kuingia Tanzania. “Tunasikia ushirikiano ushirikiano lakini wallahi mtu bora upate safari ya kutoka Mombasa kwenda Canada kuliko upate safari ya kutoka Mombasa kwenda Tanga,” alisema. Alieleza safari ya kutoka Kenya kuja Tanzania katika mipaka hiyo kuna unyanyasaji mwingi na vikwazo kwa wasafiri n ahata wafanyabiashara. “Kila ninapopata safari ya kuja nchini Tanzania mara zote naomba dua zote,” alisema. Kuhusu hilo, Rais Samia alijibu atalishughulikia. Amira katika Baraza la Wanawake Dar es Salaam, Ukht Fatma Mgidi alisema wanaume ndiyo kikwazo cha uchumi wa wanawake. Kulingana na Ukhti Fatma, wanaume wengi wanasingizia dini kuwazuia wanawake kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo, jambo ambalo ni kinyume na taratibu za imani ya Kiislamu. “Mwanaume anatumia ubabe wa kumzuia mkewe kwa kisingizio cha dini na wanawake kwa kuwapenda sana wenza wao wanakaa chini na hatimaye wanahsindwa kupanda maendeleo,” alisema. Ukht Fatma alisema wapo wanawake wenye ngazi mbalimbali za taaluma zenye uhitaji katika jamii, lakini kwa sababu wanaume zao wanawazuia kufanya kazi, wanaishia kukaa nyumbani. Hata hivyo, alitaka taasisi za fedha zitengeneze mazingira rahisi kwa wanawake kupata mikopo, ikiwemo kuwapunguzia masharti.
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imeazimia mambo 16 ikiwemo kuongeza suala
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imeazimia mambo 16 ikiwemo kuongeza suala la Bandari kuwa sehemu ya operesheni yake. Kutokana na maazimio hayo, operesheni ya chama hicho ya '+255 Katiba Mpya' kwa sasa itajulikana kama '+255 Katiba Mpya, Okoa Bandari Zetu.' Oparesheni +255 Katiba Mpya ilizinduliwa Mei 17, mwaka huu ikilenga kikuhuisha chama hicho kuanzia ngazi ya chini na kuhamasisha umma juu ya kuidai Katiba Mpya. Uamuzi wa mabadiliko ya jina la operesheni hiyo, umetokana na kile kilichoelezwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuwa, ni hatua ya kuhamasisha umma kuupinga mkataba wa Bandari. Mkataba huo ni ule wa ushirikiano (IGA) kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai juu ya uwekezaji na uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, ambao Juni 10, mwaka huu Bunge liliazimia kuupitisha. Upinzani kuhusu mkataba huo, unatokana na kile kinachoelezwa na wadau kuwa, baadhi ya vipengele vyake vinapoka maslahi ya nchi na wananchi wake. Hata hivyo, mara kadhaa Serikali kupitia viongozi mbalimbali imeeleza kilichosainiwa ni makubaliano ya awalu na si mkataba halisi, jambo linalopingwa vikali na wadau wakisema mkataba huo ndiyo muelekeo wa uwekezaji na unapaswa kufutwa. Maazimio 16 ya Chadema, yalitangazwa jana na Mbowe, katika Ofisi za Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari. Mabadiliko ya oparesheni hiyo ni miongoni mwa maazimio hayo, itakayozinduliwa Julai 28, mwaka huu mkoani Kagera na kuendelea katika Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara. Kwa mujibu wa Mbowe, baada ya Mikoa hiyo, watapumzika kwa siku kadhaa kisha kuendelea na oparesheni katika Mikoa ya Kanda ya Nyasa na hatimaye Pwani yote kwa ujumla. "Tunakusudia kuifanya nchi nzima na itazinduliwa kwa kwenda kutangaza namna CCM na Serikali yake inavyonajisi nchi kwa mikataba isiyo na tija kwa kizazi cha leo, kesho na keshokutwa. “Tumesema tunakwenda kuonana na wananchi, itoshe kusema mwambao wote wa Pwani tutaugusa tutakutana taifa zima," alisema Mbowe. Azimio lingine la Kamati Kuu kwa mujibu wa Mbowe ni kufutwa kwa mkataba huo na alisisitiza kuwa, chama hicho kitafanya kila namna kuhakikisha Serikali inalitekeleza hilo. "Msimamo wa Chadema ni kwamba mkataba huu ufutwe wote, aidha tutatumia njia mbalimbali ndani na nje ya nchi kuhakikisha mkataba unafutwa na maslahi ya nchi yanalindwa," alisema. Mbali na kufutwa mkataba, Mbowe alisema kamati kuu hiyo iliazimia bunge lifute azimio lake la kuridhia mkataba huo kwa kuwa hauna maslahi kwa nchi. Alieleza kamati kuu iliazimia Serikali iwachukulie hatua kwa mujibu wa sheria, watu wote walioshiriki kuingiza nchi katika mkataba huo usiorekebishika na unaolidhalilisha taifa. "Kamati Kuu inaunga mkono jitihada mbalimbali za wananchi kupinga mkataba huo, ikiwemo walioamua kufungua kesi katika mahakama," alisema Mbowe. Maazimio mengine ni kushirikiana na wananchi bila kujali itikadi zao katika kupinga mkataba huo na kuwahimiza kuona haja ya kudai Katiba Mpya. "Ikiwa Bunge na Serikali hazitachukua hatua, Chadema itaanzisha na kuhamasisha umma kuchukua hatua kali dhidi ya Serikali hadi itakapochukua hatua," alisema. Kulingana na Mbowe, Kamati Kuu imeridhika kwamba hakuna maslahi ya nchi na haikubaliki kwa taifa na kwamba mkataba huo unatoa haki kwa Dubai na unwaiwajibisha Tanzania. Kamati Kuu hiyo kulingana na Mbowe, imebaini mkataba huo haurekebishiki bila kubadilishwa wote kwa makubaliano ya pande zote mbili. Alieleza kamati kuu hiyo imeridhika kuwa mkataba huo unakwenda kinyume cha Katiba na sheria za nchi na Kimataifa na umesababisha Serikali kuwasilisha bungeni muswada wa mabadiliko ya sheria ya kumiliki maliasili za nchi. "Kamati Kuu imejiridhisha kuwa hakuna utafiti wa kisayansi na uliochapishwa kwa umma kuthibitisha ufanisi duni wa Bandari zetu na ubora wa DP World, Bali kila kitu kilifanywa kwa siri," alisema. Alisema Kamati Kuu imejiridhisha kuwa wananchi hawajui asili wala shabaha ya mkataba na wao ndiyo waathirika wa maamuzi hayo. Azimio lingine alilitaja ni kutokuwepo utafiti wa kisayansi wa kuonyesha njia mbadala ya kuongeza ufanisi wa bandari na kwamba ingefanyika hivyo ingesaidia wananchi kulinganisha faida na hasara za uwekezaji. Hata faida za kifedha zinazozungumzwa, alisema Kamati Kuu imejiridhisha kuwa hazikufanyiwa utafiti wowote na hata utafiti unaothibitisha unyeti wa bandari kwa usalama wa taifa umezingatiwa kabla ya kuingiwa kwa mkataba huo, pia haukufanyika. Alisema kama kuu imejiridhisha kuwa kabla ya kuingia katika mkataba huo, Serikali haikufanya uchambuzi wa kisiasa, kiuchumi na kijamii na ingefanyika hivyo kusingekuwa na mjadala. “Kamati Kuu imejiridhisha kuwa Serikali, Bunge na CCM imekurupuka na kujaribu kuficha mabaya ya mkataba na sasa inagombana na wananchi na kutumia nguvu kwa ushawishi haramu badala ya kujibu, inaibua maswali magumu zaidi kila inapojitetea. “Pia kamati kuu imebaini mchakato wa kufikia makubaliano haukufuata kanuni za kisheria, kisiasa na hata kitaaluma na hata utaratibu wa kujibu hoja za wananchi haufuati mchakato sahihi,” alisema.
Hatua ya Serikali kuanza mchakato wa mabadiliko ya sheria ikiwemo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, imei
Hatua ya Serikali kuanza mchakato wa mabadiliko ya sheria ikiwemo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, imeibua maswali kutoka kwa wadau, wakihoji kipi kilipaswa kutangulia kati ya tume na Katiba Mpya. Wamekwenda mbali zaidi, wakifananisha kuanza na mchakato wa sheria ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ni sawa na kutanguliza mkokoteni mbele ya punda au mtoto kumzaa mama. Hoja hiyo ya wadau inatokana na hatua ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuvitumia barua vyama vya siasa, ikiviomba maoni na mapendekezo ya mabadiliko ya sheria nne nchini. Sheria hizo ni ile ya Taifa ya Uchaguzi, sheria mpya ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani, marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa sura ya 258 na marekebisho ya sheria ya gharama za uchaguzi sura ya 278. Hoja ya wadau kutaka uanze mchakato wa Katiba Mpya itakayochukua nafasi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inatokana na ukongwe wa hitaji hilo ambalo hadi sasa lina umri wa zaidi ya miaka 30 tangu kuanza kwa mfumo wa siasa za vyama vingi mwaka 1992. Akizungumza na gazeti hili jana, Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika alienda mbali na kusema ama kuanza na Katiba mpya au marekebisho ya Katiba ili kutibu matatizo ya kiuchaguzi. Chadema ambacho ni chama kikuu cha upinzani, kilishaweka msimamo kupitia kwa viongozi wake wakuu kwamba hakitakubali kuingia katika uchaguzi mkuu 2025 kupitia Katiba ya mwaka 1977 yenye maudhui ya chama kimoja. Mchakato huo wa mabadiliko ya sheria za uchaguzi, umekuja wakati wadau wa uchaguzi vikiwamo vyama vya siasa kikiwamo Chadema, wakishikilia msimamo kuwa mwaka 2020 hapakuwa na uchaguzi mkuu bali haukuwa huru na haki. Lakini kabla ya uchaguzi huo, kulifanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019, nao kama ulivyokuwa uchaguzi mkuu uliibua kilio cha wagombea wa upinzani kutotendewa haki na kuifanya CCM kushinda kwa zaidi ya asilimia 90. Katika chaguzi zote hizo, baadhi ya wabunge,madiwani, wenyeviti wa mitaa na vijiji walipita bila kupingwa baada ya wagombea wa upinzani kuenguliwa huku mawakala wa baadhi ya vyama vya siasa wakiondolewa vituo vya kupigia kura. Mbali na kuenguliwa kwa wagombea, lakini kuliibuka vikundi vya kihalifu ambavyo vilifanya matukio ya utekaji wa baadhi ya wagombea, kuwapiga na kuwajeruhi wafuasi wa vyama hivyo huku baadhi wakikatwa masikio. Kwa hiyo kutungwa kwa sheria mpya ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni ishara ya kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi na pia marekebisho ya sheria mbalimbali za uchaguzi kunaweza kuwa mwanzo wa kuelekea kwenye uchaguzi huru. Tayari Machi 29 mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania ilibatilisha vifungu vya sheria vinavyoruhusu wagombea kupita bila kupingwa, kuwa vifungu hivyo vinakiuka ibara ya 21 (1) na (2) vya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977. Kilichomo barua ya Msajili Kulingana na barua hiyo, iliyotumwa Julai 10, mwaka huu kwa vyama vya siasa, “Ofisi ya waziri mkuu, Sera, Bunge na Uratibu imetuomba tuwafahamishe kuwa Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria mpya na marekebisho ya sheria zinazosimamia na ofisi ya Msajili….”inasema. “Zoezi hilo linatokana na mapendekezo ya Kikosi kazi kilichoratibu maoni ya wadau yanayohusu Demokrasia ya Vyama vingi vya siasa nchini na wadau wengine wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa,”Inaeleza barua hiyo. Barua hiyo iliyotiwa saini na Sisty Nyahoza kwa niaba ya Msajili wa Vyama vya Siasa, imewataka Makatibu wakuu wa vyama hivyo kuwasilisha maoni au mapendekezo ya marekebisho ya sheria hizo kwa mujibu wa miongozo iliyopo. Maoni na mapendekezo hayo yanatakiwa yamfikie Msajili kabla ya Julai 20,2023. Miongoni mwa mambo ya kuyazingatia katika kutoa maoni hayo ni pamoja na kubainisha jina la Tume ya Uchaguzi, kuainisha majukumu ya Tme ya Uchaguzi na kuanisha utaratibu wa uteuzi na utenguzi wa wajumbe wa Tume ya Uchaguzi. Mambo mengine ni kubainisha chanzo cha fedha za uendeshaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Shughuli za Uchaguzi, kuanzisha muundo wa Utumishi wa tume hiyo na kuipa Tume mamlaka ya kutunga kanuni, miongozo na maelekezo. Katika marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa, mambo ya kuzingatia ni pamoja na kuweka sharti kwamba mtu ambaye amepatikana na hatia ya kosa la udhalilishaji wa jinsia asiwe kiongozi wa chama cha siasa hapa Tanzania. Pia maoni hayo yazingatie kuruhusu fedha za ruzuku kugawanywa kwa vyama vya siasa kwa kuzingatia idadi ya kura za ubunge, idadi ya wabunge na madiwani ambao kinao kwa wakati husika na siyo kura za ubunge au madiwani. Chadema, NCCR-Mageuzi wafunguka Akizungumza jana, Mnyika alisema matatizo ya kiuchaguzi ni ya kikatiba hivyo marekebisho ya sheria ya uchaguzi hayawezi kuyatatua kabla ya kuanza kwanza na ama katiba mpya au marekebisho ya katiba ya 1977 kabla ya kupokea maoni. “Kutaka maoni kuhusu marekebisho ya sheria ya uchaguzi ni kurudia kazi ambayo ilishafanywa na kikosi kazi, hivyo ni mbinu ya kuchelewesha kuanza kwa mchakato wa Katiba mpya,” alisema Mnyika kupitia ujumbe wake mfupi wa maandishi. “Pia hii ni kukwepesha haja ya kufanyika kwa marekebisho ya mpito ya kikatiba kuwezesha uchaguzi huru na haki. Katika wakati muafaka Chama kitatoa tamko la kina juu ya hatua hii ya msajili wa vyama vya siasa yenye nia mbaya,”alisema. Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itifaki na Mambo ya Nje wa chama hicho, John Mrema alisema hawana mpango wa kushughulika na barua hiyo. Sababu ni kile alichoeleza kuwa, ujumbe wa chama hicho upo kwenye mazungumzo na Serikali kuhusu masuala hayo na kwamba leo, Mwenyekiti, Freeman Mbowe atazungumza na Watanzania kueleza hatua iliyofikiwa. “Kesho (leo) Mwenyekiti (Mbowe) atazungumzo kuhusu maazimio ya Kamati Kuu na mojawapo ni kuhusu hatua ya mazungumzo yetu na Serikali ilipofikia,” alisema. Kwa upande wake, kiongozi wa NCCR-Mageuzi, Joseph Selasini alisema wadau wa demokrasia ni wengi hivyo wangependa ukusanyaji wa maoni uhusishe watanzania kwa sababu sheria hizo na maamuzi yake yatawagusa watanzania. “Watanzania kwa mujibu wa Katiba wanapiga kura kuchagua viongozi na wanaweza kupigiwa kura. Sasa vyama vya siasa haviwezi kuwa na umiliki wa haki hiyo peke yao. Ni muhimu watanzania waulizwe kwa sababu hili litawahusu” “Kwa sababu malalamiko ya watanzania ni kuwa tunapiga kura lakini kura zetu haziendi kwa tuliowachagua. Vile vile zile taratibu za kuelekea upigaji wenyewe unakuwa hauonyeshi kwamba ni mchakato unaoleta uchaguzi huru na haki” Selasini alisema tangu mwanzo, maoni ya NCCR-Mageuzi yamekuwa kwamba Tume ya Uchaguzi haiwezi kuwa huru tu kwa sababu tu ya kuondoa watu wa serikali (wakurugenzi) kwenye hiyo Tume halafu wakaingizwa wakuu wa Idara. “Hata wale ni watu wa Serikali wanaweza wakatumika kupokea maagizo ambayo yanaweza kuwanyima watu haki. Sisi tunapendekeza iundwe Tume kama tulivyoshiriki uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1955,”alisema. “Ni lazima nafasi hizo za kuwa wasimamizi wa uchaguzi zitangazwe watu waombe na wachunguzwe na wapatikane watu ambao hawako upande wa serikali au vyama fulani ni kiwepo chombo cha kikatiba cha kufanya usaili,”alisisitiza. Selasini alisema haiwezekani kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa Rais kuendelea kuteua mwenyekiti wa Tume au makamishina wa Tume kwa kuwa ni lazima wataendelea kuchagua makada wenzao, jambo ambalo linalalamikiwa. Muda uliotolewa kwa ajili ya vyama vya siasa kutekeleza hilo, kwa upande wa CUF zinatosha kutokana na kile kilichoelezwa na Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano wa chama hicho, Mohammed Ngulangwa kwamba hakuna mawazo mapya yanayokwenda kutolewa. Kinachopendekezwa, alisema ni kile kile ambacho mara zote vyama vya siasa vimekuwa vikipendekeza hata kupitia michakato mbalimbali ya kutoa maoni kikiwemo kikosi kazi. “Muda unatosha kwa sababu mapendekezo tunayotakiwa kutoa yanaendanana na kile tulichokuwa tunakutaka na kukizungumza mara nyingi, kwa hiyo hakuna kitu kipya,” alisema. Hata hivyo, alisema kilicho cha vyama vya siasa ni kuharakishwa kwa michakato ya mabadiliko, hivyo atashangaa akisikia chama kinalalamikia muda uliotolewa ni mchache. “Kwa kuwa tumekuwa tukizungumza haya mambo muda mrefu na tunajua tulichokuwa tunataka kurekebishwe, hata siku moja ingetosha,” alisisitiza. Kulingana na Ngulangwa, tayari CUF imeshapokea barua hiyo kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa tangu, juzi na kwamba hivi karibuni wanatarajia kukaa kikao kwa ajili ya kuijibu na kuiwasilisha. Alisema hatua hiyo ni dalili njema za kuyafikia yale waliyoyatarajia ikiwemo tume huru ya uchaguzi, lakini aliitahadharisha Serikali kutorejea ilichokifanya katika mchakato wa Katiba Mpya wa mwaka 2014 na kusababisha kukwama. “Tulikuwa kwenye matarajio ya kupata Katiba Mpya lakini mwishoni mchakato ulikwama, hatutarajii na hiki kinachofanyika sasa kiwe mkakati wa kutuliza kelele zilizopo,” alisema Ngulangwa. Hatua hiyo, kwa upande wa ACT Wazalendo ni matumaini ya kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi, ingawa inatia shaka kwanini yahitajike maoni ambayo tayari yalishatolewa. Mwenyekiti wa chama hicho, Juma Duni Haji alisema ACT Wazalendo kupitia majukwaa mbalimbali ilishatoa maoni kuhusu namna inavyotaka tume huru ya uchaguzi iwe. “Tunaona kama kuna hatua zinachukuliwa lakini nakumbuka tulishawahi kupeleka maoni yetu hata kwenye kikosi kazi, yalikuwa maoni mengi mno,” alisema. Kwa upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu alisema wamepokea taarifa hiyo kwa faraja na tayari walishawaagiza wanasheria wao kuwasilisha maoni yao. “Ni imani yetu kwamba mchakato huu utakamilishwa mapema ili sheria mpya katika maeneo husika zipatikane kabla ya mwaka huu kuisha ili uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka ujao ufanyike chini ya tume huru ya uchaguzi,” alisema. Alieleza kazi hiyo inafanywa na jopo la wanasheria watano wa chama hicho. Akizungumzia hilo, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga alisema kinachofanyika ni jambo jema na inaonyesha nia ya dhati ya marekebisho ya sheria hizo. “Kwa sababu Rais (Samia Suluhu Hassan) alishaelekeza kuwepo na uhuru wa mikutano ya kisiasa, sheria kubadilishwa na mchakato wa Katiba kuanza na vyote hivi vinafanyika, ni dalili nzuri,” alisema. Kwa kuwa uchaguzi bado, alisema muda uliopo ni sahihi kwa ushauri na kwamba wanachokisubiri ni wakati wa kushirikishwa ili nao watoe maoni yao,” alisema. Mhadhiri wa Rasilimali Watu na Utawala, Dk Lazzaro Swai alisema jambo muhimu ni kusimamiwa kwa mchakato huo kuhakikisha kinachotarajiwa kinapatikana. “Jambo muhimu ni kuutawala na kuusimamia mchakato ili utoe muelekeo sahihi kwa kile kinachotarajiwa,” alisema. Lakini, kwa hatua iliyofikiwa, alisema inaonyesha dalili njema kwa kuwa kanuni na taratibu zimefuatwa katika utekelezwaji wake. “Hakuna sababu ya kuwa na hofu haki ya vyama vya siasa kushirikishwa na tunaona vimeshirikishwa, kila jambo linapaswa kuwa na mahali pa kuanzia na tumeona hili limeanza vizuri,” alisema.
Huenda kusuasua kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kulichagizwa na mambo matano ikiwemo janja
Huenda kusuasua kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kulichagizwa na mambo matano ikiwemo janjajanja katika matumizi ya kadi za wanachama wa mfuko huo. Kulingana na NHIF, kadi 1,346 zimekamatwa zikitumika na wasio wanachama wala wanufaika wa mfuko huo, ikielezwa kuwa wameazimwa na wanachama. Hayo yamebainika kupitia uhakiki wa wanachama uliofanywa na NHIF kuanzia Juni 1, mwaka huu katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro na Dodoma. Uhakiki huo unafanyika ikiwa ni mwaka mmoja, tangu wadau kuibua wasiwasi wa kuwa huenda mfuko huo ukafilisika, kutokana na mwenendo mbaya wa uendeshaji wake. Hofu ya kufilisika kwa mfuko huo, ilitokana na kile kilichowahi kuelezwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2021/22. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, NHIF ilivilipa vituo vya afya madai yasiyo ya kweli kiasi cha Sh14.46 bilioni kwa kipindi cha mwaka 2019/20 hadi 2021/22. Wakati fedha hizo zikipotea, CAG alibaini watumishi 146 wakiwemo 129 wa vituo vya afya na 17 wa mfuko huo walijihusisha na vitendo vya udanganyifu. “Watumishi 146 wa NHIF na wa vituo vya afya walijihusisha na vitendo vya udanganyifu, lakini Kitengo cha Kupambana na Udanganyifu kiliripoti maofisa 17 tu wa Mfuko waliojihusisha na vitendo vya udanganyifu kwa kamati za nidhamu,” alisema CAG. Akitoa taarifa ya uhakiki wa wanachama jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Benard Konga alisema uchambuzi unafanyika kujua gharama za matibabu zilizotumiwa na watu hao. Alisema iwapo zitajulikana, wanachama watapaswa kuzilipa pamoja na hatua nyingine za kisheria watakazochukuliwa. “Kila tulipobaini hilo, tulimnyang’anya mtu huyo kadi na kubaki nayo kisha kutoa taarifa kwa mwanachama aje kuifuata kadi yake ofisini,” alisema. Uhakiki huo, alisema umebaini uwepo wa wanachama 2,490 walioacha kadi zao vituoni. Kutokana na hilo, Konga alisema uchunguzi unaendelea kubaini iwapo ni watoa huduma waliotaka wanachama waache kadi ili watengeneze madai baadaye au wanachama wenyewe wamesahau. “Nitoe rai kwa wanachama kuhakikisha unaposaini baada ya kupata huduma chukua kadi yako na kwa watoa huduma iwapo mwanachama amesahau ni jukumu lao kutupa taarifa sisi ili tuzifuate na kumrejeshea mwanachama,” alisema. Jambo lingine lililobainika kutokana na uhakiki huo ni kudurufiwa kwa kadi za wanachama, akisema baadhi hutoa nakala na kwenda nazo katika vituo vya kutolea huduma. “Hilo limebainishwa wazi kuwa ni kinyume na mikataba yetu, kwamba mwanachama atibiwe kwa kadi halisi atakayokuja nayo,” alisema. Alisema uhakiki huo, ulibaini baadhi ya watoa huduma kutozingatia taratibu za uhakiki wanachama kabla ya huduma, jambo linalosababisha wasiostahili kuhudumiwa. Lingine lililobainika ni ule mtindo wa mtu kumtuma ndugu, jamaa au rafiki kwenda kumchukulia dawa. “Kwamba mimi naumwa, nampa ndugu yangu kadi yangu aende kunichukulia dawa, miongozo ya tiba inataka daktari amuone mgonjwa ndiyo atoe tiba,” alisema. Kulingana na Konga, kadi 3,589 zimebainika kuwa na taarifa zenye mashaka na kwamba wanachama wanapaswa kwenda katika ofisi za NHIF kwa ajili ya kuzihuisha. Mkurugenzi huyo alisema uhakiki huo umesababisha NHIF kusitisha kutoa huduma kwa taasisi 88 ambazo waajiriwa wake wengi wamehusika katika makossa yaliyobainishwa. “Kwa hiyo taasisi kama 88 tayari wao tumesitisha kuwapa huduma na tumeshawataarifu, tunakaa nao mezani na kama wanataka kuendelea tutawapa masharti lakini wanapaswa kuwa walinzi wa mfuko,” alisema. Katika kudhibiti janjajanja, alisema matumizi ya alama za kibaiolojia kama vidole na sura yanatarajiwa kuanza. Hata hivyo, alisema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita mfuko huo ulisitisha mikataba 48 ya watoa huduma waliofanya biashara katika hali ya ujanja ujanja. Pamoja na mikataba hiyo, alisema wataalamu wa huduma za afya 139 walichukuliwa hatua mbalimbali kulingana na sheria na miongozo ya nchi. Kadhalika, wanachama 1,197 walichukuliwa hatua mbalimbali ikiwemo kusitishiwa matumizi ya kadi zao, kulipia gharama na kuripoti katika vyombo mbalimbali vya uchunguzi. Akizungumzia hilo, Rais wa Tanzania Health Summit, Dk Omary Chillo alisema ulaghai wa wanachama inaweza kuwa moja ya sababu za hasara katika mfuko huo, ingawa zipo nyingine zinazochagiza hilo. “Hii inaweza kuwa moja ya sababu, lakini zipo na nyingine. Kweli kumekuwepo na wanachama wasio waadilifu hawaaminiki wanawapa wenzao kadi wanazitumia kinyume na utaratibu,” alisema.
Swali wanalojiuliza Watanzania kutoka maeneo mbalimbali kwa sasa ni kwanini Bandari ya Dar es Salaam
Swali wanalojiuliza Watanzania kutoka maeneo mbalimbali kwa sasa ni kwanini Bandari ya Dar es Salaam si tegemezi la kikanda pamoja na kuzungungwa na fursa lukuki. Kimkakati, bandari ya Dar es Salaam ipo katika nafasi nzuri la kuhudumia nchi nyingi kwa gharama nafuu na hatimaye kuipa faida kubwa kulinganisha na washindani wake. Hata hivyo, kushindwa kupata mbia sahihi na wa kimkakati kwa miaka mingi kumekwamisha juhudi za Bandari ya Dar es Salaam kuongeza ufanisi na mchango wake katika Pato la Taifa (GDP) na kuongeza ajira. Hapa ndipo kampuni ya DP World yenye makao mkuu yake nchini Falme za Kiarabu, inapokuja kutoa mwelekeo sahihi na hatimaye kuziba ombwe lililokuwepo. Juni 10 mwaka huu, Bunge la Tanzania lilijadili na kupitisha azimio la kupitisha Makubaliano ya Serikali (IGA) kati ya Tanzania na Dubai, kwa ajili ya ushirikiano katika uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam, yanayofuatiwa na hatua ya utekelezaji. Hatua hii itaongozwa na Makubaliano ya Serikali Mwenyeji na Makubaliano ya Ukodishaji yatakayotiwa saini baada ya mwaka mmoja wa majadiliano kuhusu maeneo ya ushirikiano kama inavyotarajiwa katika IGA. Kusainiwa kwa IGA, hata hivyo, kulipokelewa kwa hisia tofauti, huku baadhi ya Watanzania wakiunga mkono nia ya Serikali ya kuikaribisha DP World na wengine wakipinga. Wanaounga mkono DP World wanasema kampuni hiyo itaongeza thamani ya bandari ya Dar es Salaam, huku wengine wakisema si afya kwa taifa kuiacha bandari hiyo mikononi mwa wageni. Katika maelezo yake ya haraka, Wakili wa Serikali Mwandamizi wa TPA, Kulwa Sukari alisema si bandari nzima itakayoendelezwa na kuendeshwa na DP World. “Ushirikiano wetu utakuwa katika kuendeleza na kuendesha baadhi ya maeneo tu ya bandari. Utekelezaji wake utaongozwa na makubaliano ya mradi yatakayotiwa saini baadaye,” alisema Sukari. Alisema ikiwa yote yatafanyika kwa mujibu wa IGA, DP World itapewa eneo la 0-7 kati ya 12. "Serikali itaendeleza miundombinu na DP World itanunua vifaa na kufunga mifumo ya kisasa," alisema Sukari. Hii itafungua njia ya uboreshaji wa ufanisi wa bandari ya Dar es Salaam na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji wa kikanda. Kuimarika kwa ufanisi katika bandari ya Dar kutakuwa chachu kubwa kwani inakabiliwa na ushindani unaoongezeka kutoka kwa bandari nyingine za Afrika Mashariki na Kusini kama vile Mombasa, Durban, Beira na Walvis Bay. Bandari hizo hushindana kwa biashara kutoka mataifa ya Afrika kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Rwanda, Uganda, Burundi, Zambia, Malawi na Zimbabwe. Wafanyabiashara wa DRC na Zambia ambao wamekuwa wakisafirisha madini kupitia Bandari ya Dar es Salaam, kwa mfano, walikuwa walihamia katika bandari ya Durban. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa alisema Tanzania inataka bandari zake ziwe na ushindani wa kutosha ili kushindana na zile za nchi jirani. Akizubgumza katika jukwaa la Club House siku chache zilizopita, Mbossa alisisitiza ingawa bandari ya Dar es Salaam ilikuwa na nafasi ya kushughulikia kontena 12 pekee kwa saa, Mombasa ya Kenya ilikuwa ikihudumia kontena 35. Durban ya Afrika Kusini kwa upande mwingine, ilihudumia kontena 55 kwa saa. "Kile ambacho Serikali kwa sasa inajaribu kufanya ni kuweka mazingira ya ushindani wa bandari zetu ili kushindana na majirani zetu," alisema Mbossa. Kwa mujibu wa takwimu za TPA, bandari ya Dar ilihudumia tani milioni 20.43 pekee katika mwaka wa fedha 2021/22, huku mizigo ikichukua asilimia 38.2 pekee. Hii inaonyesha kuwa asilimia 61.8 ya shehena ni ya matumizi ya ndani. Hata hivyo, bandari hiyo bado haijatumia uwezo uliopo wa nchi zisizo na bandari kwa kiwango cha juu zaidi. Hata hivyo, wadau wa bandari waliliambia Mwananchi wiki iliyopita kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kufanya vizuri zaidi na kufikia lengo la tani milioni 56.34 mwaka 2032/33. "Tuna soko kubwa kuliko uwezo wetu wa kushughulikia wateja wetu na ndiyo maana tunachukua hatua kadhaa ili kuvutia wateja wapya na kuhifadhi waliopo," alisema Mbossa. Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alisema Serikali inahitaji uwekezaji wa Sh4 trilioni katika bandari ya Dar es Salaam ili kuongeza ufanisi wake. "Serikali haiwezi kufanya hivyo peke yake na ndiyo maana tunahitaji sekta binafsi kuingilia kati," alisema Msigwa. Tena, ujio wa DP World unatazamiwa kuongeza sehemu ya Malawi, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kutokana na kupunguzwa kwa tozo za mizigo kutoka $12,000 hadi kati ya $6,000 na $7,000 kwa kontena linalosafirishwa kwenda nchi hizo. Kwa mujibu wa takwimu za TPA, DR Congo ndiyo mteja mkubwa zaidi wa Bandari ya Dar es Salaam, inayovutia karibu tani milioni tatu za mizigo, ikifuatiwa na Zambia yenye tani milioni 2 na Rwanda kwa takriban tani milioni 1.5. Lakini hiyo haitoshi, ikiwa bandari ya Dar es Salaam itaongeza ufanisi wake, hisa za nchi katika masoko hayo zitapanda. Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dar es Salaam, Dk Lufunyo Hussein, aliliambia Mwananchi kuwa kuna uwezo mkubwa ambao haujatumiwa ambao ungepatikana iwapo bandari ya Dar ingekuwa inafanya kazi kwa ufanisi. "Ndio maana Serikali ilikuwa inafanya kila iwezalo kuvutia wawekezaji ambao wataongeza ufanisi na kuifanya bandari ya Dar kuwa ya ushindani. “Tanzania inahudumia asilimia mbili au tatu tu ya shehena ya Uganda kila mwaka. Hii inatuambia kwamba tunahitaji kurekebisha njia zetu za kufanya biashara, ili kuvutia mizigo zaidi,” alisema Dk Hussein. Uganda inasalia kuwa mshirika mkuu wa kibiashara wa Kenya huku bidhaa zake nyingi zinazouzwa nje na uagizaji zikipitia Mombasa. Hii inaonyesha kuwa Tanzania ina mlima wa kupanda ili kuvuna hisa za Mombasa katika shehena za Uganda. Tukija kwenye swala la DRC, hili ni moja ya soko linaloweza kuwa la Dar es Salaam na Mombasa, bandari kubwa zaidi katika Afrika Mashariki, macho yao yote yanalitazama. Tanzania, hata hivyo, ina faida zaidi ya Kenya, lakini ikiwa tu njia yake itakuwa ya ushindani kuliko ya Kenya. Mambo kama vile ushuru wa barabara, urahisishaji wa usafiri ni baadhi ya mambo ambayo wasafirishaji watatumia kuamua njia ambayo wangetaka kutumia. Sababu ya Tanzania kuunga mkono ni kwamba kuingia kwa DRC katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuna uwezekano wa kuhamisha sehemu ya mizigo kutoka ukanda wa kaskazini hadi barabara kuu ya kati. Ukanda wa kati wenye urefu wa kilomita 1,300, unaanzia katika Bandari ya Dar es Salaam na kuhudumia nchi za Tanzania, Zambia, Rwanda, Burundi, Uganda na Mashariki mwa DRC. Kwa upande mwingine, ukanda wa kaskazini, ambao una urefu wa kilomita 1,700, unaanzia Bandari ya Mombasa na kuhudumia Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Mashariki mwa DRC. Wakati DRC itakapoingia, lengo sasa litakuwa kati ya Bandari ya Mombasa na ile ya Dar es Salaam huku madereva wa mizigo wakipima njia ya kutumia katika kuvusha bidhaa hadi jimbo kubwa la DRC. Mfanyabiashara Rostam Aziz alisema iwapo bandari ya Dar es Salaam inapaswa kuongeza ufanisi, kwa kuipa kandarasi kampuni ya kimataifa ili iweke mazingira ambayo watumiaji wasiwe na hofu kama ya sasa. Kwa mfano, Zambia, alisema katika miaka ya 1960 na 1970 ilipitisha bidhaa zake katika Bandari ya Dar es Salaam kwa asilimia 100. Leo, ni asilimia 25 tu ya bidhaa zinazoagizwa na zinazouzwa nje ya nchi zinapita katika Bandari ya Dar es Salaam na asilimia 75 zinakwenda kilomita 1,200 huko Durban Afrika Kusini. Wako tayari kutumia fedha nyingi zaidi kwa ajili ya bidhaa zao kujaribu kukwepa Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kutokuwa na mifumo inayoweza kuongeza ufanisi. "Binti yangu anafanya biashara ya parachichi huko Mafinga, lakini anaamua kusafirisha kontena la mazao hayo kupitia Bandari ya Mombasa akitumia dola 12,000 kwa sababu akipitisha Dar es Salaam parachichi litaharibika kabla ya kufika sokoni," alisema. Bandari ya Dar es Salaam yenye ufanisi, alielezea, ingemgharimu Dola za Marekani 6,000 ambayo ni nusu ya dola 12,000 zilizotumika wakati wa kusafirisha nje kupitia Bandari ya Mombasa. Alipongeza pia, iwapo bandari hiyo ingekuwa na ufanisi angewapa wakulima Sh600 kwa kilo moja ya mazao kwa ajili ya usafirishaji kupitia Bandari ya Dar es Salaam.
Dhana ya uendelezaji na uendeshaji wa Bandari na ushiriki wa sekta binafsi ni mfumo wa kisasa unaotu
Dhana ya uendelezaji na uendeshaji wa Bandari na ushiriki wa sekta binafsi ni mfumo wa kisasa unaotumika katika bandari nyingi Duniani. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa nyakati tofauti imechukua hatua za kushirikisha sekta binafsi katika shughuli za kibandari. Hatua hii ilianza mwaka 2000, wakati ambao TPA kipindi hicho iliiitwa THA na Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC), iliingia mkataba na Kampuni ya Kimataifa ya Kuhudumia Makasha (TICTS). Aidha, mpango kabambe wa uendelezaji wa Bandari nchini wa mwaka 2022, unaeleza na kupendekeza kwa Serikali kuhusu namna ambayo TPA itafikia azma yake ya kuwa mmiliki na/au muendelezaji wa bandari nchini na kukasimisha shughuli za uendeshaji kwa sekta binafsi ili kuongeza ufanisi wa Bandari nchini. Serikali imeshauriwa kufanya hivyo kwa kufanya urekebishaji wa muundo wa TPA. Hatua hizi za ushirikishaji wa sekta binafsi ni muhimu katika kuhakikisha kwamba TPA inafikia azma ya uanzishwaji wake wa kuwa msimamizi wa bandari kama Sheria ya kuanzishwa kwake ilivyoelekeza. Matokeo ya ushirikishaji wa sekta binafsi Sekta binafsi ina utaalamu wa uendeshaji wa shughuli za bandari unaotokana na uzoefu wa kufanya shughuli hizo katika maeneo mengine duniani. Kutokana na uzoefu huo hasa katika teknolojia na utaalamu, sekta binafsi ina uwezo wa kuongeza ufanisi wa utoaji huduma za bandari iwapo itapewa fursa ya kufanya hivyo na hivyo kuleta manufaa yafuatayo. Kupunguza muda wa meli kusubiri nangani kutoka siku tano hadi masaa 24, kupunguza muda kwa kupakia na kupakua makasha kutoka siku 4.5 hadi siku mbili, kupunguza muda wa uondoshaji wa shehena bandari kutoka saa 12 hadi saa moja kufuatia maboresha ya mifumo ya TEHAMA. Pia, itapunguza gharama ya usafirishaji wa shehena kutoka Dola za Marekani 12,000 hadi kati ya Dola za Marekani 6,000 na 7,000 kwa kasha linalokwenda Malawi, Zambia au Jamhuri ya Demokrasi ya Congo. Kadhalika, kuongeza shehena itakayohudumiwa na bandari kutoka tani milioni 18.41 za mwaka 2021/22 hadi tani milioni 47.57 mwaka 2032/33, kuongeza mapato ya Serikali ya Kodi ya Forodha kutoka Sh7.76 trilioni za mwaka 2021/22 hadi Sh26.7 trilioni mwaka 2032/33. Si hivyo tu, sekta binafsi itafanikisha kuongezeka kwa ajira zinazotokana na shughuli za bandari kutoka 28,990 mwaka 2021/22 hadi ajira 71,907 sawa na ongezeko la asilimia 148. Kuongezeka kwa mitambo yenye Teknolojia ya kisasa ya kuhudumia makasha, kuendeleza eneo la Bandari Kavu kwa kuweka miundombinu ya kisasa ya kuhudumia aina zote za shehena, kusimika mifumo ya kisasa ya TEHAMA kwa shughuli za bandari na kuwaunganisha wateja. Pia, mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa TPA katika Bandari zote na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine za kiuchumi zikiwemo Kilimo, Mifugo na Uvuvi, kadhalika kuchagiza viwanda na biashara na ukuaji wa sekta ndogo ya usafirishaji wa reli. Faida nyingine ni kuhamisha maarifa na ujuzi kupitia mafunzo na tafiti kwa kushirikiana na vyuo vya sekta ya uchukuzi Matokeo hasi ya ushirikishwaji wa sekta binafsi Serikali kwa vipindi tofauti imechukua jitihada za kuwekeza katika miundombinu na vifaa ili kuboresha ufanisi na tija katika sekta ndogo ya bandari. Hata hivyo kutokana na urasimu mrefu wa maamuzi, jitihada hizo zimechukua muda mrefu kutatua changamoto zilizopo katika sekta ndogo ya bandari. Kwa kuzingatia hali hiyo, Serikali isiposhirikisha sekta binafsi, ufanisi na utendaji wenye tija katika bandari utaendelea kukosa ushindani katika maeneo yafuatayo. Uwekezaji katika kuendeleza miundombinu na vifaa utaendelea kuwa duni na kuathiri utendaji wa Bandari na kulikosesha taifa mapato. "Bandari zetu zitaendelea kukosa ushindani kutokana na meli kutumia muda mrefu nangani na gatini ikilinganishwa na Bandari shindani katika ukanda wetu na kuifanya bandari ya Dar es Salaam kulishwa shehena na bandari shindani," anasema Mbossa. Anaeleza bandari za Tanzania zitaendeshwa bila mifumo ya kisasa ya TEHAMA inayofungamanisha shughuli za bandari pamoja na wadau, pia zitakuwa na utendaji duni kutokana na kukosekana kwa mitambo ya kutosha na kisasa ya kuhudumia shehena. Kulingana na Mbossa, hata gharama za mizigo inayohudumiwa na bandari zetu zitaendelea kuwa kubwa kutokana na ufanisi duni wa huduma za bandari kwani meli zinatumia muda mrefu nangani na gatini na kuathiri mnyororo wa sekta ya usafirishaji. "Taifa litakosa fursa ya kuhamisha maarifa, ujuzi na stadi za kazi kutoka kwa wawekezaji hasa fursa ya kujengea uwezo vyuo vyetu vya mafunzo katika sekta ya uchukuzi, kuchelewesha matumizi ya fursa za kiuchumi zitokanazo na uwepo wa bandari ikiwa ni pamoja na ajira kwa vijana wa kitanzania. "Kampuni ya ndani kama wazabuni, wigo wa mapato ya fordha na kodi mbalimbali na kuchagiza sekta nyingine za uchumi na kukosa fursa ya kuongeza ukubwa wa soko la kuhudumia mzigo kutoka nchi jirani hasa ukizingatia uwezo na mikakati fungamanishi ya mwekezaji katika kutafuta masoko na kutoa suluhisho la jumla katika mnyororo wa usafirishaji," anasema. HISTORIA FUPI NA UWEZO WA DP WORLD Katika mahojiano hayo, Mbossa aliielezea DP World kuwa kampuni iliyoanzishwa kama mwendeshaji wa bandari wa ndani wa jiji la Dubai kati ya mwaka 1979 hadi 1998 na baadaye ilikua hadi kufikia kuwa mwendeshaji wa bandari wa kikanda kati ya mwaka 1999 hadi 2004. Ukuaji huo, anasema uliendelea hadi kufikia kuwa mwendeshaji wa bandari wa dunia, hatua iliyofikia sasa. Kwa mujibu wa Mbossa, taarifa za utendaji wa DP World zinaonesha ni kampuni inayoshika nafasi ya tano kati ya waendeshaji wakubwa wa bandari duniani na imekuwa ikihudumia takribani asilimia tisa ya shehena yote ya makasha inayosafirishwa duniani. Aidha, anasema kampuni hiyo inaendesha bandari 190 duniani katika nchi 68 zilizopo ndani ya Mabara sita duniani. Anataka huduma zinazotolewa nakampuni hiyo katika uendeshaji wa bandari maeneo mbalimbali duniani. Anasema uendeshaji wa bandari na vitengo mahsusi mbalimbali vya bandari kama vitengo makasha, mzigo mchanganyiko, mafuta na vitengo vya magari. "Uendeshaji wa Maeneo Huru ya Kiuchumi na usafirishaji wa shehena majini na utoaji huduma kwa meli baharini," anasema. Hata hivyo, anasema, "muunganiko wa huduma zinazotolewa na DP World na uendeshaji wa bandari kwa namna ambavyo kampuni hiyo imekuwa ikitoa huduma katika maeneo mbalimbali duniani, umekuwa chachu ya ukuaji wa uchumi wa nchi hizo kwa sababu za ufanisi mkubwa unaopatikana wakati wa utoaji wa huduma zenye muunganiko wa kuanzia usafirishaji wa shehena majini na nchi kavu, huduma katika bandari pamoja na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali katika Maeneo Huru ya Kiuchumi." Anasisitiza kampuni hiyo inatoa huduma za bandari katika nchi zaidi ya 70 duniani zikiwemo Korea, China, Australia, Vietnamu, Pakistani, Saudi Arabia, India, Indonesia, Brazili, Argentina, Chile, Canada, Uingereza, Ufaransa na Ubelgiji. Kwa upande wa Afrika, anasema DP World ina uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika uendeshaji wa bandari kwa nchi sita ambazo ni Algeria (Aligiers, Djen Djen), Somaliland (Berbera), Senegal (Dakar), Angola (Luanda), Msumbiji (Maputo) na Rwanda (Kigali). Hata hivyo, anasema uendeshaji wa huduma za bandari katika nchi za Afrika umeleta mchango chanya katika ukuaji wa uchumi wa nchi hizo kutokana na kuongezeka kwa ufanisi wa bandari husika na usafirishaji wa mizigo kutoka nchi moja kwenda nyingine.
Kauli mbalimbali zinazotolewa na Balozi Ali Karume kukituhumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwamba hakun
Kauli mbalimbali zinazotolewa na Balozi Ali Karume kukituhumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwamba hakuna demokrasia imezidi kuibua sintofahamu kuhusu mustakabali wake. Balozi Karume ambaye ni mwanachama wa chama hicho kwenye tawi la Mwera, katika kipindi cha miezi kadhaa sasa amekuwa akitoa shutuma dhidi ya chama hicho ikiwemo ile ya kutoshinda kwa haki kwenye chaguzi mbalimbali. Hata hivyo, tuhuma hizo dhidi ya uchaguzi zimeshindwa kuthibitishwa kwani, chombo chenye mamlaka ya kusimamia uchaguzi nchini (NEC- kwa Tanzania Bara na ZEC- kwa Zanzibar) kwa mujibu wa Katiba ndio hutangaza washindi halali. Juzi Balozi Karume ambaye alipewa onyo Juni 15, mwaka huu na Tawi la CCM Mwera kutokana na kauli zake hizo, amezirejea tena akisema kuwa yuko tayari kutetea msimamo wake huo mahali popote atakapoitwa. Kupitia video zake (Mwananchi linazo) Balozi Karume alidai kuwa, “Hakuna demokrasia ni vurugu tu, tunakwenda kwenye uchaguzi ili wabadilishane madaraka wenyewe kwa wenyewe, kwa sababu haiwezekani tukafanya uchaguzi chama kingine kikashinda kura zikahesabiwa alafu uchaguzi wote ukafutwa, kwahiyo kama demokrasia haipo ni haipo tu si kwasababu amesema yeye." Hoja za Balozi Karume zinakuja huku kukiwa na kumbukumbu ya makada kadhaa waliowahi ama kuonywa au kufukuzwa uanachama wa CCM kwa kwenda kinyume. Miongoni mwa waliowahi kufukuzwa ni Hayati Bernard Membe, Sophia Simba na Jesca Msambatavangu, kisha baadaye waliomba uanachama na kurejeshwa. Abdulrahman Kinana ambaye sasa ndiye makamu mwenyekiti wa CCM Bara aliwahi kupewa onyo la karipio, pamoja naye alionywa aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa chama hicho, Yusuph Makamba wote kwa sababu ya kile kilichoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu. Hata hivyo, kauli hizo za Balozi Karume zimeonekana kuzidi kuwa mwiba kwa CCM ambayo kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Dk Mohamed Said Dimwa kimesema kuwa hatua dhidi yake zitajulikana baada ya vikao. Akizungumza na Mwananchi jana, Dk Dimwa alisema ingawa hakusikia kilichozungumzwa na mwanadiplomasia huyo, chama hicho kiliketi kikao cha maadili jana na mwenendo wa Balozi Karume ni moja ya ajenda zilizozungumzwa. “Mimi siyajui hayo aliyoyasema, lakini sasa hivi (jana) tuna kikao cha maadili na moja ya mambo tunayozungumza ni kuhusu yeye (Balozi Karume),” alisema. Hata hivyo, alisema uamuzi wowote wa CCM hufanywa kwa vikao, hivyo chochote kuhusu kada huyo kitaamriwa na kikao. “Tusubiri vikao kisha tutachukua hatua kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya CCM, kwa hiyo ndugu mwandishi vumilia kidogo,” alisema. Mbali na kikao cha saa 7 mchana kama alivyoeleza Dimwa, alisema kingine cha Kamati Maalum kitafanyika jioni ya jana visiwani humo na kufuatiwa na kikao cha Sekretarieti jijini Dodoma leo, akisisitiza baada ya hapo lolote litajulikana. “Kesho (leo) nipigie simu nitakuwa Dodoma kwa kikao cha sekretarieti nitakupa maelezo mazuri ya kilichofanyika,” alisema. Vyama vya siasa Akizungumzia hilo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, alisema hoja hizo ni sahihi na zimezungumzwa nao mara kwa mara. “Ni sahihi na ni hoja ambazo tunazizungumza mara kwa mara, yeye kusema anasema kitu anachokijua na ukizingatia ni vitu ambavyo tumekuwa tukivizungumza, kwahiyo CCM inapaswa kujitathmini," alisema. Mwalimu alisema wananchi wanachukulia kwa uzito maneno hayo na njia pekee ya kushugulikia madai ya Karume ni kuwa na Tume huru ya Uchaguzi na mifumo ya uchaguzi yenye kuaminika. Alisema kama matakwa hayo hayatazingatiwa bado wataendelea kuamini hakuna uchaguzi huru na haki na madai ya Ali Karume yataendelea kuwa na mashiko. Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Juma Duni Haji alisema mara nyingi wamekuwa wakisema Tanzania haina demokrasia hata kabla ya kauli za Balozi Karume. "Hakuna demokrasia ni vurugu tu, tunakwenda kwenye uchaguzi ili wabadilishane madaraka wenyewe kwa wenyewe, kwasababu haiwezekani tukafanya uchaguzi chama kingine kikashinda kura zikahesabiwa alafu uchaguzi wote ukafutwa, kwa hiyo kama demokrasia haipo ni haipo tu si kwasababu amesema yeye," alisema. Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Hamad Masoud Hamd alisema kama demokrasia haipo ndani ya CCM wanapaswa kupambana. "Kama demokrasia hakuna watajua wenyewe sisi tuliopo nje huwa tukisema haipo haipo kwa hiyo wapambane wenyewe watajuana," alisema Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi alishauri madai kuhusu demokrasia ndani ya vyama yanapaswa kufanyiwa utafiti ndani ya vyama husika ndipo atafutwe yeye kama mlezi. “Nakwambia hivyo nina maana yangu, siwezi kujibu kwa simu, anza kwenye chama husika,” alisema. Anaakisi maoni ya Watanzania Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa, kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Hadija Mwendah alisema maoni hayo ya Balozi Karume yanaakisi mtazamo wa Watanzania wengi. Kulingana na Dk Hadija, si Balozi Karume pekee anayeshuku ushindi wa CCM katika chaguzi mbalimbali, alieleza wananchi wengi wamekuwa wakizungumza hayo. “Kauli anazotoa zinaakisi maoni ya Watanzania wengi na yeye mbali na ukada wa CCM ni Mtanzania, kwa hiyo kufanya hivyo ni haki yake,” alieleza. Mwanazuoni huyo alisisitiza hoja yake hiyo, akirejea yanayozungumza na Balozi Karume hasa kuhusu mashaka ya ushindi wa CCM katika uchaguzi, akisema kauli ya mwanadiplomasia huyo ndiyo uhalisia wa chaguzi nyingi Afrika. “Chaguzi nyingi za Afrika hazina ushindani na zinaturudisha kwenye mfumo ambao hatutarajii utokee, katika kipindi hiki ambacho tunajinasibu kuwa tunafuata misingi ya demokrasia,” alisema. Aliihusisha hoja yake hiyo na kilichotokea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, akisema ni vigumu kumweleza mtu kwamba Tanzania ni nchi ya demokrasia kwa hali ilivyo sasa bungeni. “Mtu atakushangaa ukimwambia Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, maana bungeni karibu wabunge wote wanatokana na chama kimoja,” alifafanua Dk Hadija. Kwa mujibu wa mwanazuoni huyo, ingawa falsafa za sayansi ya siasa zinaeleza huwezi kuwa na demokrasia bila uchaguzi, alieleza kuwepo uchaguzi si kigezo kinachojitosheleza kwamba kuna demokrasia. “Afrika kwa sehemu kubwa tunafanya uchaguzi kuonyesha umma kwamba zimefanyika, lakini kuna mianya mingi tumeiacha ili kutimiza demokrasia, bado hatujafikia,” alisema. Kwa sababu ya mazingira hayo, Dk Hadija alisema umefika wakati wananchi wanaona kura zao hazileti mabadiliko na hazina maana, ndiyo maana ni wachache wanaoshiriki kupiga kura, akirejea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. “Balozi Karume ameakisi maoni ya Watanzania wengi kwa sababu wamesoma na wanaona,” alieleza. Kwa upande mwingine, mwanazuoni huyo alisema chama cha siasa si jukwaa ambalo watu wote lazima wafanane namna ya kufikiria na kutenda. “Wanaweza kufanana kwa itikadi lakini wakatofautiana namna ya kutekeleza hiyo itikadi, kwa hiyo watu wasimtazame vibaya Balozi Karume,” alisema. Mtazamo wa Dk Hadija hautofautiani na Revocatus Kabobe mhadhiri msaidizi wa sayansi ya siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), aliyesema anachokifanya Balozi Karume ni haki yake ya kikatiba. “Ijulikane kwamba Balozi Karume ana haki ya kikatiba ya kutoa maoni yake na kujieleza,” alieleza. Lakini, kwa upande mwingine, alibainisha kauli hizo za Balozi Karume hasa kuhusu mashaka ya ushindi wa CCM katika uchaguzi, zinaongeza wasiwasi wa hicho kinachoshukiwa. “Balozi Karume amekuwa kiongozi mwandamizi wa CCM, leo hii anapokuja na shutuma dhidi ya chama hicho, tunapata wasiwasi kwamba pengine hoja za upinzani kutilia mashaka ushindi wa chama hicho katika uchaguzi ni sahihi,” alisema. Ni wakati wa Watanzania kupewa nafasi wazungumze, kwa kile kilichoelezwa na Kabobe kuwa bado kuna changamoto katika mifumo ya uchaguzi nchini. “Kama wa nje wamekuwa wakilalamikia ushindi wa CCM, leo hii mtu wa ndani anaeleza hay ohayo, bila shaka kuna kitu hapo,” alisema. Hata hivyo, alisema malalamiko kuhusu uchaguzi ndani ya visiwa hivyo yalianza tangu ulipoanza mfumo wa siasa za vyama vingi, akisisitiza matibabu ya hayo ni Katiba Mpya. “Kauli hizi za Balozi Karume zisiishie kuangaliwa kama maoni yake, bali ziwaibue Watanzania kuongeza nguvu za kudai Katiba Mpya,” alisema. Karume: Ni msimamo Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Balozi Karume alisema hakuna kauli aliyoitoa kuidhalilisha CCM, badala yake alichokieleza ni uhalisia wa mambo yalivyo ndani ya chama hicho. Kwa mujibu wa mwanadiplomasia huyo, kauli kuhusu kutokuwepo kwa demokrasia ndani ya CCM ni msimamo wake wa kitaalamu na yupo tayari kuutetea popote atakapoitwa. Msimamo wake huo, alieleza unatokana na vielelezo vya matukio mbalimbali yaliyowahi kutokea kwenye michakato ya ndani ya chama hicho, kuelekea kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu. “Mwaka 2015, kuna mtu alikuwa na mvuto, aliwahi kuwa Waziri Mkuu (Edward Lowassa), tungemweka angeshinda urais, lakini amekatwa akawekwa mtu ambaye hajulikani katika chama, hajawahi kuwa hata Katibu wa Kata wa CCM. “Lakini kikao kikamteuwa, yule yule tuliyemkataa akaenda upinzani akawekwa kugombea urais, mwisho wa siku tukapata matatizo na kugawana vipande vipande. Alihoji, “Waliofanya vitendo hivyo na kusababisha vurugu na wana CCM kugawanyika walichukuliwa hatua gani.” Uthibitisho mwingine wa ombwe la demokrasia ndani ya CCM ni kile alichoeleza kuwa, kuna wakati walioshinda katika kura za maoni hawakupitishwa kugombea ubunge, walichukuliwa waliokuwa nafasi za chini. Alipoulizwa iwapo ana hofu ya kufukuzwa ndani ya CCM, Balozi Karume alijibu hafikirii kama kuna kikao chochote halali cha chama hicho kitakacholijadili hilo kwa kuwa hakukosea. “Natamani niitwe na chama changu nisikilizwe maoni yangu, tujadiliane, lakini naamini kwa kuwa nimekitumikia chama changu kwa muda mrefu, nitatendewa haki,” alisema.
Hatma ya kuadhibiwa au kusamehewa kwa Balozi Ali Karume itajulikana baada ya vikao vitatu vya Chama
Hatma ya kuadhibiwa au kusamehewa kwa Balozi Ali Karume itajulikana baada ya vikao vitatu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM), vilivyoanza jana visiwani Zanzibar na kingine kinachofanyika leo, jijini Dodoma. Katika vikao hivyo hasa vya Zanzibar, kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM visiwani humo, Dk Mohammed Said Mohammed, suala la Balozi Karume ni miongoni mwa mambo yatakayozungumzwa. Vuguvugu la ama kuadhibiwa au kusamehewa kwa Balozi Karume, linatokana na kauli zake za hivi karibuni kuishutumu CCM na viongozi wake, alizozitoa siku chache baada ya kuonywa na chama hicho. Pamoja na kuonywa na uongozi wa CCM wa tawi la Mwera Juni 15, mwaka huu, kwa kauli kuhusu chama hicho kutowahi kushinda kihalali katika chaguzi mbalimbali, mwanadiplomasia huyo juzi kilisambaa kipande cha video kinachomuonyesha akieleza hakuna demokrasia ndani ya chama hicho. Kwa muda mrefu, mwana huyo wa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume amekuwa akiibua shutuma dhidi ya chama chake cha CCM, ikiwemo ile aliyoeleza kuwa chama hicho hakikuwahi kushinda uchaguzi kwa njia ya halali. Lakini juzi pamoja na kusisitiza kauli hiyo, aliongeza kwa kusema hakuna demokrasia ya kweli ndani ya CCM. “Kinadharia (CCM) wanadai kuna demokarasia, lakini kiuhalisia imevamiwa na watu ambao sit u wanavunja katiba, wanaichezea katiba ya chama na wanapata madaraka na wanakwenda wanasema hawafuati katiba ya chama wanafuata nyingine,” alisema katika moja ya vipande vya video hizo. Pamoja na kauli za Balozi Karume kutazamwa na wana CCM kuwa ni uasi kwa chama hicho, lakini wanazuoni wa masuala ya sayansi ya siasa, wanasema zinaakisi maoni ya Watanzania wengi. Hata hivyo, alipotafutwa kuzungumzia hilo, Balozi Karume alisema haoni kosa alilolifanya na kusisitiza kuwa, kauli hiyo ni msimamo wake wa kitaalamu, yupo tayari kuutetea popote. Vikao Vitatu Akizungumza na Mwananchi jana, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk Mohammed Said Mohammed ‘Dimwa’ alisema ingawa hakusikia kilichozungumzwa na mwanadiplomasia huyo, chama hicho kiliketi kikao cha maadili jana na mwenendo wa Balozi Karume ni moja ya ajenda zilizozungumzwa. “Mimi siyajui hayo aliyoyasema, lakini sasa hivi (jana) tuna kikao cha maadili na moja ya mambo tunayozungumza ni kuhusu yeye (Balozi Karume),” alisema. Hata hivyo, alisema uamuzi wowote wa CCM hufanywa kwa vikao, hivyo chochote kuhusu kada huyo kitaamriwa na kikao. “Tusubiri vikao kisha tutachukua hatua kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya CCM, kwa hiyo ndugu mwandishi vumilia kidogo,” alisema. Mbali na kikao cha saa 7 mchana kama alivyoeleza Dimwa, alisema kingine cha Kamati Maalum kitafanyika jioni ya jana visiwani humo na kufuatiwa na kikao cha Sekretarieti jijini Dodoma leo, akisisitiza baada ya hapo lolote litajulikana. “Kesho (leo) nipigie simu nitakuwa Dodoma kwa kikao cha sekretarieti nitakupa maelezo mazuri ya kilichofanyika,” alisema. Anaakisi maoni ya Watanzania Licha ya kinachoelezwa na mwanadiplomasia huyo kwenda kinyime na chama chake, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa, kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Hadija Mwendah alisema maoni hayo ya Balozi Karume yanaakisi mtazamo wa Watanzania wengi. Kulingana na Dk Hadija, si Balozi Karume pekee anayeshuku ushindi wa CCM katika chaguzi mbalimbali, alieleza wananchi wengi wamekuwa wakizungumza hayo. “Kauli anazotoa zinaakisi maoni ya Watanzania wengi na yeye mbali na ukada wa CCM ni Mtanzania, kwa hiyo kufanya hivyo ni haki yake,” alieleza. Mwanazuoni huyo alisisitiza hoja yake hiyo, akirejea yanayozungumza na Balozi Karume hasa kuhusu mashaka ya ushindi wa CCM katika uchaguzi, akisema kauli ya mwanadiplomasia huyo ndiyo uhalisia wa chaguzi nyingi Afrika. “Chaguzi nyingi za Afrika hazina ushindani na zinaturudisha kwenye mfumo ambao hatutarajii utokee, katika kipindi hiki ambacho tunajinasibu kuwa tunafuata misingi ya demokrasia,” alisema. Aliihusisha hoja yake hiyo na kilichotokea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, akisema ni vigumu kumweleza mtu kwamba Tanzania ni nchi ya demokrasia kwa hali ilivyo sasa bungeni. “Mtu atakushangaa ukimwambia Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, maana bungeni karibu wabunge wote wanatokana na chama kimoja,” alifafanua Dk Hadija. Kwa mujibu wa mwanazuoni huyo, ingawa falsafa za sayansi ya siasa zinaeleza huwezi kuwa na demokrasia bila uchaguzi, alieleza kuwepo uchaguzi si kigezo kinachojitosheleza kwamba kuna demokrasia. “Afrika kwa sehemu kubwa tunafanya uchaguzi kuonyesha umma kwamba zimefanyika, lakini kuna mianya mingi tumeiacha ili kutimiza demokrasia, bado hatujafikia,” alisema. Kwa sababu ya mazingira hayo, Dk Hadija alisema umefika wakati wananchi wanaona kura zao hazileti mabadiliko na hazina maana, ndiyo maana ni wachache wanaoshiriki kupiga kura, akirejea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. “Balozi Karume ameakisi maoni ya Watanzania wengi kwa sababu wamesoma na wanaona,” alieleza. Kwa upande mwingine, mwanazuoni huyo alisema chama cha siasa si jukwaa ambalo watu wote lazima wafanane namna ya kufikiria na kutenda. “Wanaweza kufanana kwa itikadi lakini wakatofautiana namna ya kutekeleza hiyo itikadi, kwa hiyo watu wasimtazame vibaya Balozi Karume,” alisema. Mtazamo wa Dk Hadija hautofautiani na Revocatus Kabobe mhadhiri msaidizi wa sayansi ya siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), aliyesema anachokifanya Balozi Karume ni haki yake ya kikatiba. “Ijulikane kwamba Balozi Karume ana haki ya kikatiba ya kutoa maoni yake na kujieleza,” alieleza. Lakini, kwa upande mwingine, alibainisha kauli hizo za Balozi Karume hasa kuhusu mashaka ya ushindi wa CCM katika uchaguzi, zinaongeza wasiwasi wa hicho kinachoshukiwa. “Balozi Karume amekuwa kiongozi mwandamizi wa CCM, leo hii anapokuja na shutuma dhidi ya chama hicho, tunapata wasiwasi kwamba pengine hoja za upinzani kutilia mashaka ushindi wa chama hicho katika uchaguzi ni sahihi,” alisema. Ni wakati wa Watanzania kupewa nafasi wazungumze, kwa kile kilichoelezwa na Kabobe kuwa bado kuna changamoto katika mifumo ya uchaguzi nchini. “Kama wa nje wamekuwa wakilalamikia ushindi wa CCM, leo hii mtu wa ndani anaeleza hay ohayo, bila shaka kuna kitu hapo,” alisema. Hata hivyo, alisema malalamiko kuhusu uchaguzi ndani ya visiwa hivyo yalianza tangu ulipoanza mfumo wa siasa za vyama vingi, akisisitiza matibabu ya hayo ni Katiba Mpya. “Kauli hizi za Balozi Karume zisiishie kuangaliwa kama maoni yake, bali ziwaibue Watanzania kuongeza nguvu za kudai Katiba Mpya,” alisema. Mbona alikula nyama haram? Kinyume na maoni ya wanazuoni hao, kada wa CCM kutokea Kusini Pemba, Kassim Haji Salum alieleza kushangazwa na hatua ya Balozi Karume kuikosoa CCM ambayo imemwezesha kushika nyadhifa mbalimbali. “Kama anasema CCM haijawahi kushinda uchaguzi, kwanini alikubali uteuzi wa Rais Ali Mohammed Shein kuwa Waziri wa Vijana, ina maana alikubali kula nyama ya haram?” alihoji. Kada huyo alihusisha hoja za Balozi Karume na hasira ya kukatwa jina lake wakati wa kuwania urais wa Zanzibar, mwaka 2020. Hata hivyo, alieleza shutuma zake dhidi ya Rais wa visiwa hivyo, Dk Hussein Ali Mwinyi ni kinyume na uhalisia, kwa kuwa rais huyo amebadilisha mengi Zanzibar. Karume: Ni msimamo Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Balozi Karume alisema hakuna kauli aliyoitoa kuidhalilisha CCM, badala yake alichokieleza ni uhalisia wa mambo yalivyo ndani ya chama hicho. Kwa mujibu wa mwanadiplomasia huyo, kauli kuhusu kutokuwepo kwa demokrasia ndani ya CCM ni msimamo wake wa kitaalamu na yupo tayari kuutetea popote atakapoitwa. Msimamo wake huo, alieleza unatokana na vielelezo vya matukio mbalimbali yaliyowahi kutokea kwenye michakato ya ndani ya chama hicho, kuelekea kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu. “Mwaka 2015, kuna mtu alikuwa na mvuto, aliwahi kuwa Waziri Mkuu (Edward Lowassa), tungemweka angeshinda urais, lakini amekatwa akawekwa mtu ambaye hajulikani katika chama, hajawahi kuwa hata Katibu wa Kata wa CCM. “Lakini kikao kikamteuwa, yule yule tuliyemkataa akaenda upinzani akawekwa kugombea urais, mwisho wa siku tukapata matatizo na kugawana vipande vipande. Alihoji, “Waliofanya vitendo hivyo na kusababisha vurugu na wana CCM kugawanyika walichukuliwa hatua gani.” Uthibitisho mwingine wa ombwe la demokrasia ndani ya CCM ni kile alichoeleza kuwa, kuna wakati walioshinda katika kura za maoni hawakupitishwa kugombea ubunge, walichukuliwa waliokuwa nafasi za chini. Alipoulizwa iwapo ana hofu ya kufukuzwa ndani ya CCM, Balozi Karume alijibu hafikirii kama kuna kikao chochote halali cha chama hicho kitakacholijadili hilo kwa kuwa hakukosea. “Mimi natamani niitwe na chama changu nisikilizwe maoni yangu, tujadiliane, lakini naamini kwa kuwa nimekitumikia chama changu kwa muda mrefu, nitatendewa haki,” alisema.