query
stringlengths 17
98
| positive
listlengths 1
10
| negative
listlengths 1
16
| cluster
int64 0
60
|
|---|---|---|---|
Bandari kubwa nchini Kenya iko wapi?
|
[
"Bandari ya Kilindini\nBandari ya Kilindini ni hori kubwa asili ya maji yenye urefu kwenda chini unaoendelea barani kutoka Mombasa, Kenya. Inatumika kama bandari ya Mombasa, na inayo uendelezaji mikoani hadi Uganda na Sudan. Bandari ya Kilindini ni sehemu kuu ya Bandari ya Mombasa, bandari ya kimataifa ya pekee nchini Kenya. Inasimamiwa na Mamlaka ya Bandari ya Kenya (KPA). Mbali na upakuaji na upakiaji mizigo, bandari ya Mombasa ni hupokea meli za kitalii kwa mara nyingi.",
"Kaunti ya Mombasa\nUchumi wa Mombasa na nchi ya Kenya kwa jumla hutegemea sana bandari ya Mombasa. Bandari ya Mombasa ndio bandari kubwa zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki. Bidhaa nyingi hupitia hapo kutoka na kuingia ndani ya nchi. Bandari hii pia hutegemewa na nchi ya Uganda, Burundi, Sudani Kusini, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda kupitisha bidhaa kama vile, mafuta. \nMombasa pia ni kituo kikuu cha utalii kwa sababu ya fuko zake zenye mchanga, Fort Jesus na Mji wa Kale. Baada ya mashambulizi kadhaa ya kigaidi katika miaka ya awali ya mwongo wa 2010 na Al Shabaab na vikundi vingine, utalii ulidorora. Nchi za Marekani, Uingereza, Ufaransa pamoja na nchi zingine za magharibi zilianza kutoa tahadhari za safari. Baada ya Operesheni Linda Nchi, na juhudi za polisi kukumbana na ugaidi, juhudi zinaelekezwa kuimarisha utalii tena. Pia, kuanzishwa kwa huduma ya reli mpya ya SGR kati ya Jiji la Mombasa na Nairobi, kumeongeza idadi ya watalii wa ndani."
] |
[
"Busia, Uganda\nMji huu, pamoja na mji dada yake wa Busia, Kenya kando ya mpaka, ni vituo vya shughuli za kibiashara kubwa na trafiki ni nzito katika pande zote mbili. Bidhaa kutoka Uganda ni pamoja na mazao ya biashara kama kahawa, pamba na mbao zinazopelekwa katika bandari ya Mombasa nchini Kenya kwa ajili ya kuuza nje. Vyakula kama ndizi, mananasi na maembe zinazopelekwa kwa soko ya Kenya pia hupita mpakani. Kwa upande mwingine, Uganda huagiza mafuta ya petroli, bidhaa za viwandani na nyumbani kama mafuta ya kupikia, sabuni, nguo,vifaa vya elektronik na magari.\nBusia ndio mji wa shughuli nyingi sana mpakani kati ya nchi hizi mbili jirani wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mji wa mpaka wa Malaba ulioko takribani kaskazini, ni wa pili kwa shughuli za kibiashara kati ya Uganda na Kenya katika eneo la pamoja la mpaka wao. Tazama jadwali hapa chini:",
"Kenya\nKwa karne nyingi, upwa wa Kenya umekuwa mwenyeji wa wafanyabiashara na wasafiri. Kati ya miji iliyopo kwenye upwa wa Kenya ni mji wa Malindi. Umebakia kuwa makazi muhimu ya Waswahili tangu karne ya 14 na wakati mmoja ulishindana na Mombasa kwa ukuu pande hizi za Afrika Mashariki. Kwa kawaida, Malindi umekuwa mji na bandari ya kirafiki kwa serikali zingine. Mwaka wa 1414, Sultani Mwarabu wa Malindi alianzisha uhusiano wa kidiplomasia na utawala wa Uchina wa Ming, wakati wa safari za mchunguzi Zheng He. Katika mwaka wa 1498, utawala wa Malindi ulimkaribisha msafiri na mvumbuzi maarufu kutoka Ureno, Vasco da Gama.",
"Kenya\nNairobi inaendelea kuwa kituo muhimu na cha kimsingi kwa mawasiliano na biashara cha Afrika Mashariki. Kinajivuna kuwa na miundo msingi ya uchukuzi na mawasiliano bora zaidi katika eneo hili, na wafanyi kazi wenye ujuzi. Makampuni mengi ya kigeni hudumisha matawi yao katika eneo hili ama ofisi za kuyawakilisha mjini Nairobi. Mnamo Machi 1996, Marais wa Kenya , Tanzania na Uganda waliifufua Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC). Shabaha za EAC ni pamoja na kasawazisha kodi na ada zinazotozwa bidhaa, utembeaji huru wa watu na kuimarisha miundo msingi katika eneo hili. Nchi hizi tatu za Afrika Mashariki zilitia saini mkataba wa Customs Union Agreement mwezi wa Machi 2004.",
"Kenya Ports Authority\nKenya Ports Authority \"(KPA)\" ni shirika la serikali lenye wajibu wa \"kudumisha, kutekeleza, kuboresha na kusimamia kufanyika kwa huduma zote kwenye Bahari ya Hindi ukanda wa pwani ya Kenya, ikiwa ni pamoja na Bandari ya Kilindini hususan ya Mombasa. Bandari zengine zinazohudumiwa na KPA ni pamoja na Lamu, Malindi, Kilifi, Mtwapa, Kiunga, Shimoni, Funzi na Vanga. KPA ilianzishwa mwaka wa 1978 kwa kitendo cha Bunge na iko Mombasa.",
"Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki\nHifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki ni moja ya hifadhi kubwa zaidi na kongwe nchini Kenya iliyo tambaa eneo la kilomita za mraba 11,747. Ilifunguliwa mnamo Aprili 1948, na iko karibu na kijiji cha Voi katika Wilaya ya Taita Mkoa wa pwani. Hifadhi hii imegawanywa katika sehemu za mashariki na magharibi na barabara na reli ya A109. Jina lake ambalo linatokana mto Tsavo, ambao unatiririka kutoka magharibi hadi mashariki kupitia hifadhi hii, iko mpakani mwa mbuga ya kitaifa ya milima ya Chyulu, na hifadhi ya wanyama ya Mkomazi nchini Tanzania.",
"Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta\nUkumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta au Kenyatta International Conference Centre (KICC) ni jengo la ghorofa 30 iliko mjini Nairobi, Kenya.\nIko katikta eneo la kati la biashara la Nairobi. Ni ukumbi kwa mikutano, maonyesho na matukio maalumu ndani ya umbali wa kutembea wa hoteli kadhaa za nyota tano. Imekuwa mwenyeji wa mikutano mingi ya kimataifa na semina.\nKuna vyumba kadhaa vya mikutano vilivyo na vifaa vizuri na kile kikubwa kabisa kiko na uwezo wa zaidi ya wajumbe 4,000. Iko na vifaa vya kutafsiria lugha sambamba ambavyo vina uwezo wa kutafsiria lugha saba, kituo cha biashara cha kisasa, benki, huduma za ziara na kusafiri, kiwanja kikubwa na pahali pa kuegezea magari salama.",
"Utalii nchini Kenya\nHifadhi ya taifa ya Nairobi ilikuwa mbuga ya kwanza nchini Kenya ilipoanzishwa mwaka wa 1946. Iko takriban kilomita 7 kusini mwa katikati ya Nairobi, mji mkuu wa Kenya, na ni ndogo ikilinganishwa na mbuga nyingine za wanyama barani Afrika. Majumba marefu jijini Nairobi yaweza kuonekana kutoka kwenye mbuga.",
"Bandari ya Kilindini\nWakati wa Vita vya II vya dunia, wakati Kenya ilikuwa koloni ya Uingereza, Kilindini ilikuwa makao ya muda ya wigo wa Mashariki ya jeshi la Uingereza mapema Avril kutoka 1942 hadi tishio la Ujapani kwa mji wa Colombo, Ceylon (sasa Sri Lanka) ulikuwa umeondolewa. Karibu, afisi buku ya Mashariki ya Mbali, kituo cha mbali cha Waingereza cha kuvunja kanuni iliyokuwa Bletchley Park,ulihifadhiwa katika shule ya Allidina Visram, Mombasa na ilikuwa na mafanikio katika kuvunja kodi za kibaharia za Kijapani.",
"Kenya\nMombasa ulikuwa mji wenye bandari wa nchi ya Kenya kabla ya ukoloni katika Enzi ya kati. Bandari hiyo ilitumika kuendeleza biashara na miji mingine yenye bandari Afrika, Uajemi, na wafanyabiashara Waarabu, Yemeni na hata Bara Hindi.",
"Bandari\nKuna mabandari yanayopokea mizigo ya kila aina kama bandari ya Dar es Salaam au Mombasa."
] | 15
|
Je,mji mkuu Australia ni gani?
|
[
"Mji mkuu\nAustralia ilijenga mji mkuu mpya kwa sababu miji mikubwa ya Sydney na Melbourne yote yalitaka kuwa mji mkuu wa kitaifa wa Shirikisho la Australia. Mwaka 1908 eneo la Canberra lililokuwa mashambani wakati ule liliteuliwa, ujenzi wa mji mpya ulianza mwaka 1913 na serikali pamoja na bunge ilihamia Canberra mwaka 1927. Dola la shirikisho la New South Wales lilikabidhi \"Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho\" lililokuwa eneo la pekee chini ya Bunge la Australia moja kwa moja.",
"Canberra\nCanberra ni mji mkuu wa Australia mwenye wakazi 330,000. Si sehemu ya jimbo lolote la shirikisho la Australia lakini \nlimepewa eneo lake la kitaifa kando la mto Molonglo ndani ya eneo la jimbo New South Wales.",
"Australia\nMji mkuu, Canberra (wakazi milioni 308,700) ulijengwa kati ya Sydney na Melbourne kwa sababu miji hiyo miwili ilishindwa kukubaliana kati yao ni mji upi unaostahili kuwa mji mkuu."
] |
[
"Kisiwa cha Krismasi\nKisiwa cha Krismasi ni eneo dogo la Australia katika Bahari Hindi takriban 500 km upande wa kusini ya Jakarta mji mkuu wa Indonesia na 2,400 km kaskazini ya Australia yenyewe.",
"Brisbane\nBrisbane ni mji mkubwa wa tatu wa Australia na mji mkuu wa jimbo la Queensland katika kaskazini ya nchi. Idadi ya wakazi ni mnamo 1,730,000. Iko kando la mto Brisbane na mdomo wake unapita mjini.",
"Abidjan\nAbidjan ni mji mkubwa nchini Cote d'Ivoire pia ni mji mkuu hali halisi. Vilevile ni bandari kuu ya nchi kwenye Ghuba ya Guinea ya bahari ya Atlantiki. Abidjan haiko baharini moja kwa moja lakini kwenye wangwa ya Ebrie inayotengwa na bahari kwa kanda nyembamba ya mchanga.",
"Australia ya Magharibi\nAustralia ya Magharibi (Kiing.: \"Western Australia\") ni moja ya jimbo 8 ya kujitawala ya Jumuiya ya Australia. Idadi ya wakazi wake ni takriban 2,163,200. Mji wake mkuu ni Perth.",
"Abuja\nAbuja ni mji mkuu wa Nigeria. Idadi ya wakazi wake imekadiriwa kuwa watu 178,462 . Mwaka wa 1976, serikali ya Nigeria iliamua kuanzisha mji mkuu mpya badala ya Lagos. Wakachagua katikati ya nchi, na mipango ya ujenzi ikaundwa chini ya makampuni matatu ya Marekani: PRC Corporation; Wallace, McHarg, Roberts na Todd; na Archisystems. Mipango hiyo ikabadilishwa baadaye na Kenzo Tange, msanifu majengo maarufu wa Japani. Abuja ikatangazwa rasmi kuwa mji mkuu wa Nigeria tarehe 12 Desemba 1991. Iko mahali pa 9, 10, Kaskazini na 7, 10, Mashariki.",
"Miji bora\nNi mji wa Australia ulioshika nafasi ya 10; ni mji wenye vivutio vingi kama vile ufukwe, mipango mizuri ya ujenzi na bandari, daraja kubwa la kwenda angani, pia limekuwa kivutio cha utalii.",
"Wikimania\nMpaka kumwisho kulikuwa na miji mita, na miji mingine ya Atlanta na Cape Town. Andiko kwa ajili ya mji wa Karlsruhe, London na Toronto pia iliwasilishwa na baadaye walijiondoa wenyewe kwenye kinyang’anyilo. Kulikuwa na mkukanganyiko, ilifikia hata watu kutaka kugomea kuhudhuria Wikimania 2008 kwa sababu ya Egypt's ikituhumiwa kuendesha zoezi la kuhakiki na kuwaweka watu magerezani kwa sababu ya kuanzisha mitandapo wakati wa utawala wa Rais Husein Mubaraka wa nchi hiyo. era. Mohamed Ibrahim, mhitimu wa Alexandria University ambaye alifanya kazi kubwa ya kupeleka mkutano huo katika jiji la Alexandria, aliongea kupitia kituo cha redio cha BBC \"akisema “ nafikiri tuna haki ya kuendelea na kuwa na uhuru wa kujieleza katika kiwango cha juu.\" moja ya lengo lake ilikuwa ni kukuza lugha ya kiarabu Arabic Wikipedia ambapo alikuwa mchangiaji mzuri tangu mwaka 2005. Waziri wa baraza la mawazi la misri ambaye alifungua mkutano kwa niaba ya rais Husein Mubaraka. \n Mkutano ulifanyika Buenos Aires, Argentina, kuanzia tarehe 26–28, August 2009. Ulihudhuriwa na washiriki 559. maamuzi ya mwisho yakuwa kati ya miji ya Buenos Aires na Toronto. Brisbane na Karlsruhe pia walipendekezwa lakini baadaye walijiondoa.\nMkutano wa ulifanyika kuanzia tarehe 9–11, July katika ukumbi wa Polish Baltic Philharmonic jijini Gdańsk, Poland. Katika siku yake ya kwaqnza ya tarehe 9 august,mkutano huo ulilenga sana katika kuzungumzia mradi wa kitaaluma waWikiSym. Tenda kwa Amsterdam na Oxford Wikimania 2010 lost by a small margin. mkutano huu ulikuwa ndo wa kwanza kujikita katika masuala ya kiutamaduni , hasa onesho la bendi ya philharmonic orchestra, wakisherehekea miaka kumi tangu kufariki kwa mwanamuziki mtunzi wa Poland Władysław Szpilman na maonyesho ya filamu ya Truth in Numbers?. Kwenye mkutano, Sue Gardner, Mkurugenzi mtendaji wa Wikimedia Foundation, alisema kwamba lengo la foundation ni kukuza ama kuongeza namba ya watembeleaji wa tovuti ya wikimedia kutoka milioni 371 na kufikia million 680 kwa mwezi katika kipindi cha miaka mitano ijayo.\nMkutano wa Wikimania 2011 Uilifanyika jijini Haifa, Israel, kuanzia tarehe 4–7, August. Ukumbi wa mikutano ulikuwa katika jumba la Haifa Auditorium Badala ya ukumbi wa Beit Hecht cultural center on Mount Carmel. Wasemaji katika mkutano walikuwa ni pamoja na Yochai Benkler, a fellow at the Berkman Center for Internet and Society katika Chuo Kikuu cha Harvard na Joseph M. Reagle Jr. wa MIT, mtunzi wa \"Good Faith Collaboration: The Culture of Wikipedia\". Mkuu wa kamati ya sayansi na teknologia wa Knesset, Meir Sheetrit, pia alipata nafasi ya kuzungumza katika mkutano huo Yonah Yahav, ambaye ni Meya wa jiji la Haifa. Mmoja wapo wa wadhamini wa mkutano walikuwa ni Chuo Kikuu cha Haifa. zaidi ya masuala 125 yalijadiliwa katika makundi manne na mkutano uklihudhuriwa na washiriki 720 Wikimedians kutoka katika nchi 56 duniani, hii ilihusisha hata nchi ambazo hazina uhusiano wa kidipromasia na Israel. katika mahojiano na Haaretz, Mwanzilishi waWikipedia Jimmy Wales alieleza kwamba kulikuwa na mgomo ulioitishwa na dhidi ya Israel, kama ilivyokuwa katika mkutano wa Misri 2008. Mgogoro baina ya wahariri kuhusiana na mgogoro wa kisiasa wa Israel-Palestinian conflict,jithada zilizokuwa zikifanywa na makundi mbalimbali ya waisraelkwa lengo la kuongeza namba ya wahariri wa Wikipedia, alisema daima wahariri wa Wikipedia hawafungamani “alisisitiza” jambo hili halina mjadala.”Wikimedia Foundation Mkurugenzi mtendaji Sue Gardner aliueleza mkutano kuhusu mwanamume mmoja kutoka nchi za mashariki namna ambavyo yeye hakukubaliana na Wikipedia ya leo. Katika sherehe ya kufunga mkutano tarehe 7 mwezi wa Augost bwn Jimmy wales alionyesha stampu ya kwanza ya mwaka ambayo ilitengenezwa maalum na shirika la posta la Israel kama heshima kwa Wikipedia ikitimiza miaka 10 tangu kuanziswa kwake mwaka 2001. Miongini mwa miradi ambayo ilijadiliwa ilikuwa ni pamoja na kushirikisha masuala ya utamaduni, Maktaba na maeneo ya makumbusho. After the conference, participants were offered a free tour of Haifa, Jerusalem, w:Nazareth:Nazareth or Akko. mwenyenykiti Shay Yakir, aliyekuwa anamaliza muda wake kwa shirika la wikimedia la Israel, alisema kwa waisrael kuandaa mkutano wa wikimania mwaka 2011 kwao ilikuwa kama kuandaa michezo ya Olimpic."
] | 51
|
Je,hadithi ya Pinokyo ilitungwa lini?
|
[
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nMambo yaliyompata Pinokyo: habari za mwanasesere (kwa Kiitalia jina linalotamkwa hivyo linaandikwa Pinocchio) ni hadithi ya karagosi hai ya ubao na shani zake. Hadithi hiyo ilitungwa na mwandishi Mwitalia Carlo Collodi tangu mwaka 1881 hadi 1883 ilipotolewa kama kitabu, kwa jina la Kiitalia \"Le avventure di Pinocchio: Storia di un burattino\"."
] |
[
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nTabia muhimu ya Pinokyo katika hadithi ni pua lake linaloanza kuwa ndefu sana kila akisema uwongo. Kutokana na hilo wachoraji wa katuni za kisiasa hupenda kumchora mtu kwa pua ndefu wakitaka kuonyesha huyu ni mwongo.",
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nSiku moja seremala Maestro Ciliegia anakuta kipande cha ubao kinachoanza kusema akitaka kukikata. Kwa kuogopa anampa rafiki yake Geppetto (jina linasomeka Jepeto) aliye mchongaji. Geppetto anatumia ubao huo kuchonga karagosi anayeendelea kusema na mara baada ya kukamilika anatoroka. Akirudi nyumbani kwa njaa anaahidi kuwa mtoto mzuri na mtiifu lakini baada ya muda anatoroka tena. Anapatwa na shani nyingi hadi kukutana na baba yake Geppetto ndani ya tumbo la nyangumi. Pamoja wanajiokoa na Pinokyo anaahidi tena kuwa mtoto mzuri na safari hii anaacha utundu wake. Baada ya kutenda mema, anaamka siku moja anajikuta amebadilika umbo lake na sasa yu mvulana mwenye mwili wa kibinadamu.",
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nCollodi alianza kutoa habari za Pinokyo kama simulizi mfululizo katika gazeti la kila wiki kwa ajili ya watoto. Hadithi ilipendwa sana na wasomaji ikamhamasisha mhariri kumwambia Collodi aiendeleze na hatimaye ikawa kitabu. Labda awali \"Pinokyo\" haikulenga watoto, na mwishowe Pinokyo alikufa vibaya wa kunyongwa kwa makosa yake mengi.",
"Pinokyo (mhusika)\nSiku moja seremala Maestro Ciliegia anakuta kipande cha ubao kinachoanza kusema akitaka kukikata. Kwa kuogopa anampa rafiki yake Geppetto (jina linasomeka Jepeto) aliye mchongaji. Geppetto anatumia ubao huo kuchonga karagosi anayeendelea kusema na mara baada ya kukamilika anatoroka. Akirudi nyumbani kwa njaa anaahidi kuwa mtoto mzuri na mtiifu lakini baada ya muda anatoroka tena. Anapatwa na shani nyingi hadi kukutana na baba yake Geppetto ndani ya tumbo la nyangumi. Pamoja wanajiokoa na Pinokyo anaahidi tena kuwa mtoto mzuri na safari hii anaacha utundu wake. Baada ya kutenda mema, anaamka siku moja anajikuta amebadilika umbo lake na sasa yu mvulana mwenye mwili wa kibinadamu.",
"Alan Paton\nRiwaya za pili na za tatu za Paton, \"Phalarope anayechelewa sana\" (1953) na \"Ah, lakini Nchi yako ni Nzuri\" (1981), na hadithi zake fupi, \"Hadithi Kutoka Eneo Lenye Shida\" (1961), zote zinahusu na mada ile ile ya ubaguzi wa rangi zilizokuwa katika kitabu cha kwanza cha mwandishi huyo. \"Ah, lakini nchi yako ni nzuri\" ilikuwa na msingi wake katika hadithi za maisha, barua, hotuba, habari na rekodi za kesi za kisheria, na wahusika wa kubuni na wa kweli kama vile Albert Luthuli na Hendrik Verwoerd. Riwaya yenyewe ilikuwa ubunifu wa kihistoria, iliyotoa maelezo yenye ufasaha kuhusu harakati za upinzani nchini Afrika Kusini wakati wa miaka ya 1960. \"Paton anajaribu kuwapa wahusika wake ubinadamu ambao hautarajiwi kutoka kwao. Katika riwaya hii, kwa mfano, tunakutana na Muafrikana mkaidi anayekiuka Sheria dhidi ya Uovu. Kuna Waafrikana wengine pia wanaaongozwa na na nia yao na si sheria, na kanuni zinazotolewa na bunge lisilokuwa na uso na lenye kushikilia mtazamo mmoja tu.\" (kutoka kitabu cha Waandishi wa Kiafrika wa baada ya Enzi ya Kikoloni,kilichohaririwa na Pushipa Naidu Parekh na Siga Fatima Jagne, 1998)",
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nLakini mhariri alimwomba kuendeleza simulizi na kuipeleka kwenye mwisho mwema kama kitabu kwa watoto. Hivyo masimulizi yaliyowahi kutolewa katika gazeti yalikuwa sehemu ya kwanza ya kitabu na Collodi aliendelea kuongeza shani mpya za Pinokyo anapokutana na roho jike mwema mwenye nywele za buluu anayemwokoa mara kadhaa katika matatizo yake.",
"Anjela wa Foligno\nMang'amuzi mengine aliyoshirikisha ni kama haya yafuatayo: “Siku moja roho yangu ilinyakuliwa, nikamuona Mungu katika uangavu mkubwa kuliko wowote niliowahi kujua… Nilimuona Mungu katika giza, na ni lazima liwe giza, kwa kuwa yuko juu mno kuliko roho, na lolote linaloweza kufikiriwa halilingani naye… Sioni kitu ila naona yote; hakika inapatikana katika giza. Kadiri giza lilivyo nene, wema unazidi yote. Ni fumbo lililofichika… Uweza, hekima na utashi wa Mungu, nilivyoviona vizuri ajabu siku nyingine, natambua ni kidogo kuliko hilo. Hilo ni kitu kizima, hivyo ni kama sehemu zake tu”. Maana yake, sasa sioni kitu maalumu, ila naona sifa zote za Mungu zimeunganika vizuri ajabu katika ukuu wake unaozidi akili yangu.",
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nHadithi ilitafsiriwa na kutolewa kwa Kiswahili mwaka 1956 na Tanganyika Mission Press mjini Tabora.",
"Mambo yaliyompata Pinokyo\nTangu 1892 kitabu kilitafsiriwa kwa lugha nyingi; kwanza kwa Kiingereza, baadaye pia kwa lugha zote za Ulaya na baadaye hata nje ya Ulaya."
] | 25
|
Timu ya taifa ya soka ya Brazil imeshinda kombe la dunia mara ngapi?
|
[
"Timu ya Taifa ya Kandanda ya Brazil\nBrazil ni timu ya taifa yenye mafanikio zaidi katika Kombe la aduni la FIFA, mashindano ya mpira wa miguu ya kimataifa, kuwa mshindi wa taji mara tano: 1958, 1962, 1970, 1994 na 2002. Brazil pia ina utendaji bora zaidi katika Kombe la Dunia, kwa kawaida na masharti kamili, na rekodi ya ushindi 73 katika mechi 109 zilicheza, tofauti ya lengo la 124, pointi 237, na hasara 18. [12] [13] Brazil ni timu ya kitaifa pekee ya kucheza kwenye matoleo yote ya Kombe la Dunia bila kutokuwepo na haja ya playoffs. pia ni timu ya kitaifa yenye mafanikio katika Kombe la Confederations ya FIFA yenye majina manne: 1997, 2005, 2009 na 2013.",
"Kombe la Dunia la FIFA\nBrazili ndio nchi pekee ambayo imeweza kutwaa kombe hilo mara tano. Ujerumani na Italia zimelitwaa mara nne. Nchi nyingine ambazo zimewahi kulitwaa ni Uruguay, Argentina, Uingereza, Ufaransa na Hispania."
] |
[
"Timu ya Taifa ya Kandanda ya Brazil\nTimu ya soka ya taifa la Brazil inawakilisha Brazili katika soka ya kimataifa ya wanaume. Brazil inasimamiwa na Shirikisho la Soka la Brazil CBF, kikundi kinachoongoza kwa soka nchini Brazil. Wamekuwa mwanachama wa FIFA tangu 1923 na mwanachama wa CONMEBOL tangu 1916",
"Bebeto\nNa alishinda mabao 39 katika mechi 75 za Brazil, Bebeto ni mchezaji wa sita wa timu yake ya taifa. Alikuwa mchezaji bora wa Brazil katika Copa América ya 1989 kama taifa liliendelea kushinda mashindano hayo. Katika Kombe la Dunia la FIFA 1994, alifanya ushirikiano mkubwa wa mgomo na Romário kuongoza Brazil kwenye robo fainali ya Kombe la Dunia. Alikuwa pia mwanachama wa upande wa Brazil ambao alishinda Kombe la Confederations ya FIFA ya 1997, wakati huohuo alishinda medali za fedha na shaba za Olimpiki na Brazil katika michezo ya Olimpiki ya kiangazi ya 1988 na 1996. Mnamo 1989.",
"Timu ya Taifa ya Kandanda ya Ubelgiji\nTimu ya taifa ya Ubelgiji imehusika katika mashindano makubwa ya mpira wa miguu ya kila baada ya miaka minne. Ilionekana katika hatua za mwisho za vikombe kumi na tatu vya FIFA ya Dunia na michuano mitano ya UEFA ya Ulaya, na ilionekana katika mashindano ya soka ya Olimpiki, ikiwa ni pamoja na mashindano ya Olimpiki ya 1920 ambayo walishinda.",
"Antonio Valencia\nValencia aliichezea timu ya taifa kwa mara ya kwanza katika mechi ya kufuzu kushiriki katika Kombe la Dunia la FIFA dhidi ya Paragwei tarehe 27 Machi 2005, na alifunga mabao mawili katika ushindi wa 5-2. Aliichezea Ecuador katika kombe la dunia la 2006, na alichaguliwa kama mteule wa timu ya FIFA ya wachezaji 11 bora, ambayo inatambua wachezaji nyota katika kila nafasi katika Kombe la Dunia. Pia aliorodheshwa kama mmoja wa wagombea sita kwa tuzo la mchezaji bora mchanga wa Gillette. Barua pepe lilisambazwa nchini Uingereza na liliwapa moyo watu kumpigia kura Valencia, katika jaribio la kuzuia Cristiano Ronaldo kushinda. Valencia alipokea idadi kubwa ya kura katika uchaguzi wa mtandao wa tarakilishi, [34] lakini tangu Mshindi wa tuzo anadhamiriwa na kura za wafuasi na jopo la majaji, hatimaye tuzo alipewa Lukas Podolski.",
"Kombe la Dunia la FIFA 2018\nTimu nyingine zilizofanikiwa kurudi baada ya kitambo kidogo ni,Misri mara ya mwisho ilishiriki 1990, Morocco tokea 1998, Peru tangu 1982 na Senegal ambayo ilishiriki mwaka 2002 na kufika hatua ya robo fainali. Ni kwa mara ya kwanza pia kwa nchi tatu kutoka “Nordic countries” na nchi nne za Kiarabu kufanikiwa kushiriki katika mashindano hayo. \nNchi maarufu zilizoshindwa kupita ni pamoja na Italia waliowahi kuchukua kombe hilo mara nne, Uholanzi, Cameroon.",
"Timu ya Taifa ya Kandanda ya Argentina\nWasimamizi wa Kombe la Dunia wa Argentina ni César Luis Menotti mwaka wa 1978, na Carlos Bilardo mwaka 1986.",
"Timu ya Taifa ya Kandanda ya Afrika Kusini\nTimu ya kandanda ya kitaifa Afrika Kusini au Bafana Bafana ni timu ya kitaifa ya Afrika Kusini na hudhibitiwa na Shrikisho la Kandanda la Afrika Kusini (SAFA). Walirudi kwenye jukwaa la dunia mwaka wa 1992, baada ya miaka ya kupigwa marufuku kutoka FIFA. Watakuwa mwenyeji wa kombe la dunia la FIFA mnamo Juni 2010 baada ya kuwa mwenyeji wa Kombe la Shirikisho la FIFA mwaka wa 2009. Afrika Kusini itakuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia la FIFA. Wao wamekuja njia ndefu kuanzia wakati walipigwa marufuku na FIFA mwaka wa 1962 na kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia.",
"München\nKlabu ya soka ya Bayern München imeshinda mara 19 kombe la kitaifa na mara tatu kombe la Ulaya.",
"Timu ya Taifa ya Kandanda ya Ujerumani\nTimu ya soka ya taifa ya Ujerumani ni timu ya soka ya mpira wa miguu ambayo imewakilisha Ujerumani katika mashindano ya kimataifa tangu mwaka 1908.\nTimu hii inaongozwa na Chama cha Soka cha Ujerumani, kilianzishwa rasmi mwaka 1900. Mwishoni mwa Kombe la Dunia la FIFA la mwaka 2014, Ujerumani ilipata kiwango cha juu zaidi cha Elo cha timu yoyote ya soka ya kitaifa katika historia na pointi 2205."
] | 16
|
Rais wa kwanza wa Gabon aliitwa nani?
|
[
"Omar Bongo\nKiongozi huyo amevunja rekodi ya kuwa Rais aliyekaa muda mrefu marakani kuliko Rais yeyote barani Afrika. Rais huyo amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 73, ambapo ameiongoza Gabon kwa miaka 42.\nBongo alijiunga na serikali ya Gabon mwaka 1965 na mwaka 1967 akawa makamu wa Rais ambapo mwaka huo huo akashika hatamu ya kuwa Rais wa nchi hiyo kufuatia cha kifo cha ghafla cha Rais Leon Mba.\nBongo alipoingia madarakani alijenga utawala imara ambao ulinufaika zaidi baada ya kugunduliwa kwa mafuta nchini Gabon ingawa utajiri wake ulinufaisha idadi ndogo ya watu wanaokadiriwa kuwa milioni 1.5. kitu kilicholeta lawama kubwa kwa kiongozi huyo.\nRais huyo amefariki dunia wakati akipata tiba ya saratani jijini Barcelona nchini Hispania.\nRais Bongo ameaga dunia takribani miezi mitatu baada ya kifo cha mkewe, Edith Lucie Bongo Ondimba (45) aliyefariki dunia 14 Machi mwaka huu wakati akipata tiba mjini Rabat nchini Morocco.\nBongo na Edith walifunga ndoa mwaka 1990. Edith aliuguzwa kwa miezi kadhaa nchini Morocco, na umma haukutangaziwa sababu za kifo chake. Edith alikuwa binti wa Rais wa Congo, Denis Sassou Nguessou. Mwanaharakati huyo wa mapambano dhidi ya Ukimwi alikuwa mke wa pili kwa Bongo, mke wa kwanza wa Rais huyo alikuwa, Josephine Nkama.",
"Historia ya Gabon\nJamhuri ya Gabon, kutoka kushinda uhuru kutoka ukoloni wa Ufaransa tarehe 17 Agosti 1960, imeongozwa na Rais watatu, Léon M'ba, El Hadj Omar Bongo ambaye amekuwa kiongozi kutoka mwaka wa 1967 hadi kifo chake (2009: ndiye aliyekuwa kiongozi barani Afrika aliyeshikilia uongozi kwa muda mrefu zaidi), halafu mwanae Ali.\nMwaka wa 1990 Gabon ilianza demokrasia ya vyama vingi na katiba ya kidemokrasia ambayo inaruhusu ukweli wa uchaguzi na utekelezaji wa idara za serikali.",
"Gabon\nJamhuri ya Gabon, kutoka kushinda uhuru kutoka Ufaransa tarehe 17 Agosti 1960, imeongozwa na Rais watatu, Léon M'ba, El Hadj Omar Bongo ambaye amekuwa kiongozi kutoka mwaka wa 1967 hadi kifo chake (2009: ndiye aliyekuwa kiongozi barani Afrika aliyeshikilia uongozi kwa muda mrefu zaidi), halafu mwanae Ali."
] |
[
"Omar Bongo\nHabari za kifo cha Rais huyo wa Gabon zilikuja wiki chache baada ya mahakama nchini Ufaransa kutaka kufanyiwa uchunguzi juu ya mali ya Rais Bongo nchini Ufaranasa. Uchunguzi kama huo pia utafanyiwa mali ya rais wa Kongo Brazzaville Dennis Sassou Nguesso na rais wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang` Nguema.\nShirika la kupambana na rushwa \"Transparency International\", tawi la Ufaransa linawalaumu viongozi hao kwa kutumia fedha za umma, kununua nyumba katika nchi za nje na pia kwa kununua magari ya kifahari, madai ambayo viongozi hao wameyakanusha.\nRipoti iliyotolewa na serikali ya Gabon ilisema kuwa, ilithibitisha kuwa rais Bongo alikuwa amelazwa katika zahanati moja nchini Uhispania lakini haikutaja chochote kuhusiana na maradhi ya saratani, baada ya madai kuwa rais Bongo alikuwa akiugua saratani ya utumbo.\nPia ripoti hiyo ilisema kuwa kiongozi huyo hajafanyiwa upasuaji wowote na kuvilaumu vyombo vya habari kwa kueneza uvumi wenye lengo la kuivuruga Gabon.",
"Omar Bongo\nEl Hadj Omar Bongo Ondimba (30 Desemba 1935 – 8 Juni 2009) alikuwa Rais wa nchi ya Gabon tangu mwaka wa 1967. Baadhi ya marais barani Afrika, Bongo ameshika urais kwa muda mrefu kabisa. Alimfuata Leon M'ba akiwa na umri wa miaka 31 tu, na wakati ule alikuwa rais kijana kabisa duniani. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa \"Albert-Bernard Bongo.\nKiongozi huyo mwanzoni alitambulika kama Albert Benard Bongo kabla ya baadae kusilimu na kuitwa Omari Bongo. baada ya kumaliza masomo yake ya awali na sekondari mjini Brazzaville, Bongo alianza kazi katika shirika la umma lililokuwa likishughulika na masuala ya posta na simu lakini baadae aliingia kwenye mafunzo ya kijeshi na taratibu ukawa mwanzo wa kujikita kwenye siasa.",
"Ghana\nKwame Nkrumah, Waziri Mkuu wa kwanza na baadaye Rais wa nchi ya sasa ya Ghana, hakuwa tu kiongozi wa Kiafrika wa kupigana dhidi ya ukoloni ila alikuwa pia mtu aliyekuwa na ndoto ya muungano wa Afrika ambayo haingejipata katika ukoloni mamboleo. Alikuwa kiongozi wa serikali ya kwanza Afrika kukuza Muungano wa Waafrika (Pan-Africanism), wazo ambalo alilipata wakati wa masomo yake katika Chuo Kikuu Cha Lincoln lililoko Pennsylvania (Marekani), wakati ambapo Marcus Garvey alikuwa anapata umaarufu kwa harakati zake za “Back to Africa Movement.\" Aliunganisha ndoto za Macus Garvey na zile za mwanachuo mashuhuri Mmarekani Mweusi W.E.B. Du Bois ili kuandaa Ghana kisasa.",
"Oliver N'Goma\nOliver N'Goma (23 Machi 1959 – 7 Juni 2010) alikuwa mpiga gitaa na mwimbaji wa muziki wa Afro-zouk na reggae kutoka nchini Gabon. Alipewa jina la utani la \"Noli,\" alizaliwa mjini Mayumba huko mjini kusini-mwagharibi mwa nchi ya Gabon mnamo mwaka wa 1959. Alifahamika sana kwa kibao chake cha mwaka wa 1989 Bane, ambacho kilivumishwa sana na Radio Africa N.1 na Gilles Obringer.",
"Burundi\nRais atachaguliwa na wananchi wote lakini mapatano yalisema rais wa kwanza atachaguliwa na bunge.\nMwaka 2005 uchaguzi wa kwanza wa bunge baada ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ulifanyika. Chama cha CNDD-FDD kilipata kura nyingi na kiongozi chake Pierre Nkurunziza alichaguliwa na bunge kuwa rais wa taifa. Vyama vya UPRONA na FRODEBU vilivyotangulia kuongoza serikali ya mpito vilipata kura chache kwa sababu vilishtakiwa kuwa na rushwa na upendeleo wa kindugu.",
"Ali Bongo Ondimba\nAli-Ben Bongo Ondimba (amezaliwa na jina la Alain Bernard Bongo mnamo tar. 9 Februari 1959) ni mwanasiasa kutoka nchini Gabon ambaye kwa sasa ni Rais wa Gabon kwa kufuatia ushindi wake kwenye uchaguzi wa rais wa 2009.",
"Thomas Sankara\nMwaka wa 1966, rais wa kwanza wa Volta ya Juu, Maurice Yameogo, aliondolewa kupitia mapinduzi na kamanda wa jeshi, Sangoulee Lamizana, alichukua uongozi. Lamizana akaanzisha chuo cha wanajeshi mjini Ouagadougou, ambacho kilikuwa cha kwanza nchini. Sankara alisikia kwenye redio tangazo kwamba wanafunzi wa kwanza wa chuo hicho watachaguliwa kutoka waliohitimu shule ya upili. Alipohitimu, alikuwa mmoja wa waliochaguliwa. Wakati huo, alikuwa na umri wa miaka 17."
] | 56
|
Nchi ya Thailand ina idadi ngapi ya watu?
|
[
"Uthai\nNchi ina wakazi zaidi ya milioni 67, hivyo inashika nafasi ya 20 duniani."
] |
[
"Mkimbizi\nKuhusiana na kuwapa makao mapya \"waliotoka\", mnamo mwaka wa 2008 wakimbizi 65,548 walipewa makao mapya katika nchi 26, ongezeko kutoka idadi ya 49,868 ya mwaka wa 2007. Idadi kubwa zaidi ya waliosaidiwa na Ubalozi wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi kutoka walikuwa kutoka nchi za Thailand (16.807), Nepal (8.165), Syria (7.153), Jordan (6.704) na Malaysia (5.865). Kumbuka kwamba hizi zilikuwa nchi za kutoka ambapo wakimbizi walipewa makao mapya, si nchi zao za kiasili.",
"Jiografia ya Tanzania\nTanzania ina idadi kubwa sana ya watu waishio nchini, kutokana na makabila mbalimbali yaliyomo nchini, yakiwemo ya Wasukuma, Wanyamwezi, Wahaya, Waha, Wagogo, Wanyakyusa, Wahehe, Wachaga, Waluguru, Wazaramo na mengineyo.",
"Mkimbizi\nWapatao wakimbizi 30,000 wa Kirohingya ni wakazi wa kambi mbili katika maeneo ya Nayapara na Kutupalong ya Cox, Wilaya ya Bazar nchini Bangladesh. Wakazi wa kambi hizi wanapata huduma za msingi, walioko nje hawapati huduma hizo. Mabadiliko nchini Burma bado yakiwa mbali, lazima Bangladesh iyafahamu mahitaji ya kipindi kirefu ya wakimbizi wote wa Kirohingya nchini, na kuyaruhusu mashirika ya kimataifa kupanua huduma ambazo zitafaidi Warohingya na vilevile jamii. Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi, UNHCR limekuwa likiwabagua wakimbizi wa Kirohingya kutoka nchini za Burma na Bangladesh.",
"Kiphu-Thai\nKiphu-Thai ni lugha ya Kitai-Kadai nchini Vietnam, Laos na Uthai inayozungumzwa na Waphu-Thai. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kiphu-Thai nchini Uthai imehesabiwa kuwa watu 470,000. Pia kuna wasemaji 187,000 nchini Laos (2005) na 209,000 nchini Vietnam (2002). Kufuatana na uainishaji wa lugha, Kiphu-Thai iko katika kundi la Kitai ya Kusini-Magharibi.",
"Tahiti\nTahiti ni kisiwa kikuu cha Polinesia ya Kifaransa. Kiko upande wa kusini-magharibi wa funguvisiwa ya Tuamotu. Eneo la kisiwa ni 1045 km². Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Faaa. Mwaka wa 2012, idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa 183,645. Watu wakaao kisiwani kwa Tahiti huongea Kitahiti.",
"Mkimbizi\nBaada ya msafara wa kutoka wa Watibeti wa mwaka 1959, kuna zaidi ya Watibeti 150,000 wanaoishi nchini Uhindi, wengi katika makazi katika Dharamsala, Mysore, na Nepal. Hawa ni pamoja na watu ambao wamekimbia kwa kuikwea milima ya Himalaya wakitoroka eneo la Tibet, wakiwa na watoto wao na wajukuu wao. Nchini Uhindi idadi kuu ya Watibeti wanaozaliwa nchini humo bado hawana uraia na wao hubeba hati iitwayo Kadi ya Utambulisho inayotolewa na serikali ya Uhindi badala ya pasipoti. Waraka huo unasema kuwa uraia wa mtu mwenye kuubeba waraka ni wa Kitibeti. Ni waraka huo ambao mara nyingi hukataliwa kama hati halali ya kusafiri katika idara nyingi za forodha na uhamisho. Wakimbizi wa Kitibeti pia humiliki Kitabu cha Kijani Kibichi kinachotolewa na Serikali ya Tibet Uhamishoni kwa haki na wajibu kuelekea utawala huu.",
"Wilaya ya Tharaka\nIdadi ya watu katika Wilaya hii kulingana na Hesabu ya 1999 ni 100,992, na hakuna wanaohesabiwa kuwa wakazi wa Mtaani.\nMnamo 1998, Wilaya hii ilitenganishwa kutoka Tharaka-Nithi, ambayo pia ilikuwa sehemu ya Wilaya Kubwa ya Meru.\nTharaka ndiyo maskani ya watu wa Ameru (Wameru) ambao wakati mwingine wanatajwa kuwa na uhusiano na kabila zingine ziishizo katika maeneo ya Mlima Kenya: Wakikuyu na Waembu.",
"Mkimbizi\nNchi yenye idadi kubwa ya waliohamishwa makwao nchini mwao ni Sudan, ambapo idadi hiyo ni watu milioni 5. Kufikia mwaka wa 2006, ikiwa na wakimbizi na watu wasiokuwa na makao 800,000. Wakazi wote walipohesabika, Azerbaijan ilikuwa na idadi kuu ya watu waliofukuzwa kutoka makwao ulimwenguni kote.",
"Indonesia\nNchi ina wakazi 238,452,952 (2004) hivyo ina nafasi ya nne kati ya mataifa makubwa duniani. Ni nchi yenye Waislamu wengi kuliko nyingine zote duniani. Makabila asili ni 300 hivi; kubwa zaidi ni Wajava (42 %).",
"Sumatra\nSumatra ni kisiwa cha Indonesia. Kiko upande wa kusini wa bara la nchi ya Malaysia. Eneo la kisiwa ni 480,847 km². Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Medan. Mwaka wa 2010 idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa 50,365,538. Watu wakaao kisiwani kwa Sumatra huongea lugha mbalimbali, idadi yake zaidi ya hamsini, hasa Kimalay na lugha nyinginezo."
] | 53
|
Nchi ya Kongo ilipata uhuru mwaka gani?
|
[
"Katanga\nBaada ya uhuru wa Kongo mwaka 1960 jimbo lilijitenga na kuwa nchi ya pekee chini ya urais wa Moise Tshombe. Jeshi la UM lilimaliza kipindi hiki kwa nguvu ya kijeshi na kurudisha Katanga kuwa sehemu ya Kongo tena hadi Januari 1963. Katika kipindi hiki kifupi waziri mkuu wa Kongo Patrice Lumumba aliuawa katika Katanga.",
"Patrice Lumumba\nMnamo mwezi wa Octoba, mwaka 1959, Lumumba, kama kiongozi wa chama cha MNC, alikamatwa kwa kosa la kuchochea vurugu za kupinga serikali ya kikoloni katika mji wa Stanleyville ambapo watu takriban 30 waliuawa na yeye alihukumiwa kwenda jela kwa muda wa miezi sita. Mnamo tarehe 18 ya mwezi Januari 1960 ambayo ilikuwa siku ya majaribio na hapohapo katika siku ya kwanza ya mkutano wa wa kuzungumzia hatma ya nchi ya kidemokrasia ya Kongo itakumbukwa kwamba licha ya Lumumba kuwa jela katika kipindi hicho cha chake cha MNC kilifanikiwa kuwashawishi wananchi kwenye uchaguzi uliofanyika mwezi Decemba na kushinda katika jamhuri ya Congo. Kutokana na nguvu ya umma iliyokuwa ikifanywa na wananchi wa Congo dhidi ya kuachiliwa kwa Lumumba kutoka kila kona, aliachiliwa na kuruhusiwa kuhudhuria katika mkutano wa Brussels. Mkutano huo ulifikia kilele tarehe 27, June 1960 kwa azimio la uhuru wa nchi ya Kongo na kupanga uchaguzi tarehe 30 ya mwaka huo huo wa 1960 Uchaguzi Mkuu wa Congo 11–25 May 1960. Lumumba na chama chake cha MNC walipata ushindi uliowawezesha kuunda serikali kwa tangazo la tarehe 23 June 1960 na Patrice Lumumba anapata cheo cha uwaziri mkuu akiwa na umri wa miaka 34 na Joseph Kasa-Vubu akiwa ndie Rais wake wa kwanza. Kwa mujibu wa katiba ya Congo mnamo tarehe 24 June serikali ilipitisha kura ya kijasiri ambayo iliamuliwa na baraza la maseneta kwamba tarehe 24 iwe ni siku ya ya kuadhimisha uhuru wa Congo.",
"Bendera ya Jamhuri ya Kongo\nIlianzishwa Agosti mwaka 1958 Kongo ilipopata madaraka ya kujitawala ndani ya Umoja wa Kifaransa ikaendelea kuwa bendera ya taifa baada ya uhuru kamili mwaka 1960.\nMwaka 1970 wakati wa Jamhuri ya Watu wa Kongo bendera ilibadilishwa kuwa bendera nyekundu yenye nyota na jembe pamoja na nyundo za njano halafu majani ya mnazi ya kijani.",
"Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo\nKoloni la Kongo ya Kibelgiji lilipata uhuru tarehe 30 Juni 1960."
] |
[
"Lubumbashi\nÉlisabethville ulitumikia kama mji mkuu na kitovu cha biashara wa Jimbo la kujitenga la Katanga wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka 1960-1963. Moise Tshombe alitangaza uhuru wa Katanga mnamo Julai 1960. Viongozi wa Kongo walimtia nguvuni akashtakiwa kwa uhaini Aprili 1961, hata hivyo alikubali kufutilia washauri wake wa kigeni na vikosi vya kijeshi kubadilishana na uhuru wake.",
"Laurent Kabila\nAlirudi 1996 wakati wa uvamizi wa Kongo ya Mashariki ya wanamigambo wa Hutu kutoka Rwanda. Mabaki ya jeshi la kihutu kutoka Rwanda walikuwa wamekimbilia Kongo 1994 baada ya mauaji ya kizazi ya Rwanda na sasa walishambulia Wabanyamulenge waliokuwa Watutsi wa Kongo. Serikali ya Rwanda ilitafuta njia ya kumaliza wanamigambo hawa kwa sababu walikuwa tishio kwa utaratibu mpya wa Rwanda. Hapa walikuwa tayari kusaidia kujenga vikosi vya Wakongo waliokuwa tayari kupambana na Wahutu katika Kongo",
"Historia ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo\nMtawala alikuwa na cheo cha Manikongo na ufalme uligawiwa kwa majimbo sita. Baada ya kufika kwa Wareno wafalme na matabaka ya juu walikuwa Wakristo. Ufalme uliporomoka kutokana na vita vilivyosababishwa na biashara ya watumwa na kuingilia kwa wafanyabiashara ya watumwa katika siasa ya ndani. Hata hivyo, nasaba za watawala waliotumia cheo cha \"Awenekongo\" waliendelea kukaa katika mji mkuu wa kale M'banza-Kongo (iliyobadilishwa jina kuitwa San Salvador) hadi mwaka 1914 ambako Wareno walifuta mabaki ya uhuru na kufanya eneo lililobaki sehemu kamili ya koloni lao la Angola.",
"Force Publique\nWakati wa uhuru wa Kongo Wabelgiji hawakufanya juhudi kuwaandaa Waafrika kwa uongozi. Hadi mwisho Force Publique ilikuwa jeshi la askari Waafrika walioongozwa na maafisa wazungu. Mara baada ya uhuru uasi wa askari waafrika ulitokea walioshambulia maafisa wazungu na uasi ulikandamizwa na wanajeshi kutoka Ubelgiji.",
"Mobutu Sese Seko\nChini ya Mobutu nchi kubwa ya Kongo-Zaire ilirudi nyuma. Mobutu alijitajirisha kupita kiasi wakati nchi yake ilioza. Mwaka 1984 mali yake binafsi nje ya Kongo ilikadiriwa kuwa dolar za Marekani bilioni 4. Nchi kubwa za Magharibi, kama vile Marekani na Ufaransa, walimvumilia na kumsaidia kwa sababu alionekana kama mwanasiasa anayepambana na Ukomunisti na harakati za ukombozi, kwa mfano Angola.",
"Kamerun ya Kiingereza\nBaada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia usimamizi wa maeneo ya kukabidhiwa ulihamia mikononi mwa Umoja wa Mataifa ulioamua ya kwamba maeneo hayo yapewe uhuru kuanzia mwaka 1960. Ilhali Kamerun ya Kiingereza ilitazamiwa kuwa ndogo mno kwa kuanzisha nchi ya pekee, pia haikuwa na eneo mfululizo, wananchi walipewa chaguo cha kujiunga na nchi jirani.",
"Patrice Lumumba\nMaadhimisho ya uhuru wa Congo kwa mara ya kwanza yalifanyika mnamo tarehe 30 June 1960 ambapo maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na Mfarme Baudouinwa Ubeljiji pamoja na vyombo mbalimbali vya habari kutoka nchi za nje. Lumumba alitoa hotuba yake kama Waziri mkuu katika nchi huru japo yeye alikuwa ameenguliwa katika ratiba ya shughuli hiyo. Hotuba ya Mfalme wa Ubeljiji Mfalme Baudouin alihutubia kwa kutukuza utawala wa kikoloni, huku akilingania fikra za mjombae ambae alikuwa mfalme wa Ubeljiji akiitwa Léopold wa Pili glossing over atrocities committed during the Taifa huru la congo. Mfalme aliendelea kutoa masharti, \"aliwataka kuto kufanya mabadiliko yoyote mpaka hapo wao watakapo ona kwamba wanaweza kufanya vyema, na kwamba hawakutakiwa kufanya mabadiliko yoyote yalika bidhiwa na kwamba tutaendelea kutoa ushauri. \" Lumumba aliufahamisha umma kwamba uhuru uliotolewa na wabeljiji sio haukuja hivihivi:"
] | 18
|
Je,msitu ipi kubwa zaidi bara Afrika?
|
[
"Msitu wa mvua\nMaeneo makubwa yako hasa Brazil katika beseni ya Amazonas, Afrika katika beseni ya mto Kongo, Asia ya Kusini-Mashariki na kaskazini ya Australia."
] |
[
"Milima ya Ufa Mashariki\nMilima ya Ufa Mashariki ni safu mbili za milima ya eneo la Maziwa makubwa ya Afrika, katika nchi a Kenya, Uganda, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Burundi.\nInaitwa hivyo kutokana na uhusiano wake na Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki; safu ya magharibi ina: Milima ya Virunga, Milima ya Mitumba na Milima ya Rwenzori, wakati ile ya mashariki ina vilele vya juu zaidi katika bara zima la Afrika: Mlima Kilimanjaro (mita 5,895, sawa na futi 19,340) na Mlima Kenya (mita 5,199, futi 17,058). Kati ya milima mingine kuna Mlima Elgon kati ya Kenya na Uganda. Yote, isipokuwa Ruwenzori ina asili ya volkeno.",
"Bara\nMabara jinsi yalivyo leo hayakuwepo tangu mwanzo wala hayakai vile. Ilhali kila bara inalingana na bamba 1 au mabamba ya gandunia ina pia mwendo pamoja na bamba lake. Wanajiolojia huamini ya kwamba miaka mamilioni iliyopita mabara yote yaliwahi kukaa pamoja kama bara 1 kubwa sana lililoendelea kupasuliwa baadaye. Vipande huelea juu ya koti ya dunia ambayo ni kiowevo na moto. Mwendo wa mabamba umepimiwa kuwa sentimita kadhaa kila mwake. Uhindi zamani haikuwepo sehemu ya Asia, na sasa hivi Afrika inaelekea kupasuliwa kwenye mstari wa bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki.",
"UEFA\nUEFA ndilo shirikisho la bara kubwa zaidi katika FIFA kwa sita yaliyomo. Kati ya mashirikisho yote, kwa mbali ndilo lenye nguvu zaidi katika masuala ya mali na ushawishi katika ngazi ya klabu. Karibu wachezaji wote mashuhuri wa soka ulimwenguni hucheza katika ligi za Uropa, kidogo kwa sababu ya mishahara inayopatikana kutoka vilabu tajiri zaidi duniani, hasa katika Uingereza, Uhispania, Italia na Ujerumani. Nyingi ya timu za kitaifa zenye nguvu zaidi duniani ziko katika UEFA. Katika nafasi 32 zilizoko katika Kombe la Dunia la FIFA 2010, 13 zilitengewa timu za mataifa ya UEFA, na kwa sasa 12 ya timu bora 20 kulingana Orodha ya FIFA ya Dunia ni wanachama wa UEFA.",
"Jiografia ya Kenya\nEneo hili la milima ndilo la juu zaidi nchini Kenya (na la pili kwa urefu barani Afrika): Mlima Kenya, unaofikia urefu wa mita 5,199 (futi 17,0570) na ni eneo lenye mito ya barafu. Ng'ambo ya mpaka wa Tanzania Mlima Kilimanjaro () huweza kuonekana upande wa kusini.",
"Umaskini\nNafasi bora za kazi katika mataifa tajiri zaidi husababisha watu wenye vipawa maalum kuhama, na hivyo kuwapoteza wataalamu. Kupotea huku kunaligharimu bara la Afrika zaidi ya Dola bilioni 4 zinazotumika kuajiri zaidi ya wataalamu 150,000 kutoka nchi za ng’ambo kila mwaka.",
"Deutsche Lufthansa\nDeutsche Lufthansa ni shirika ya ndege kubwa zaidi kwenye bara Ulaya, kulingana na jumla ya wasafiriwa inabeba. Ni ndege kuu nchini Ujerumani. Jina la kampuni hili linatokana na \"Luft\" (neno la Kijerumani linalomaanisha \"hewa\") na \"Hansa\" (baada ya \"Hanse\" iliyokuwa ushirikiano mashuhuri wa wafanyabiashara thabiti).",
"Kichomi (diwani)\nShairi la kwanza \"Jinamizi\" linatalii dhamira ya dhuluma barani Afrika. Siasa za Afrika zimekoleza msingi wa dhuluma. Kuna aina mbili za ukoloni: ukoloni mkongwe unaowakilishwa na watu weupe kwenye mtumbwi na ukoloni mamboleo unaowakilishwa na watu weusi kwenye mtumbwi. Jazanda ya mtumbwi inawakilisha nchi za Afrika. Samaki baharini ni wananchi wazalendo, majitu yenye meno ya kutisha ni wakoloni wa kisasa na mabepari wanaoendelea kulifyonza bara la Afrika. Kupitia kwa tashtiti na kejeli mshairi anaudhihaki 'utawala wa chuma' yaani utawala wa kimabavu. Mamba wanasimamia wakombozi ambao baada ya mapinduzi wanawasaliti wananchi wenzao. Hapa sanaa ya ushairi inatumiwa kama jukwaa la kutetea haki ya mnyonge katika jamii. Hata hivyo, mwelekeo na tuni inayotawala kwenye shairi hili ni ile ya utamaushi na udhanaishi. Mshairi amekata tamaa kuhusu suala la uhuru barani Afrika. Baada ya uhuru ukoloni unaendelea Afrika kwa misingi na sura mpya.",
"Madola\nKatika mabara, lile lenye nchi nyingi zaidi ni Afrika likiwa na nchi au madola 54, likifuatiwa na bara la Ulaya likiwa na madola 48, kisha Asia likiwa na madola 44, halafu Amerika ya Kaskazini pamoja na Amerika ya Kati likiwa na madola 23, na baada yake ni Australia na Pasifiki (Oshania) likiwa na madola 14, na mwishowe ni Amerika ya Kusini likiwa na madola 12. Kwa hivyo, kwa ujumla, kuna madola 195 ulimwenguni.",
"Lamu\nMji ulistawi kwenye biashara kati ya pwani la Afrika Mashariki na Bara Arabu pamoja na Uhindi. Kilwa ilikuwa kituo kwa ajili ya majahazi yaliyopita njiani. Miji yote ya Uswahilini ilinunua bidhaa kutoka Waarabu na Wahindi na kuuza pembe za ndovu, ganda la kobe na mazao pamoja na watumwa. Biashara kubwa ya Lamu ilikuwa miti aina ya mkoko yenye ubao usiooza rahisi hasa hauliwi na mchwa hivyo unafaa vizuri kwa ujenzi wa nyumba. Mikoko ilipatikana tele kwenye funguvisiwa ya Lamu lakini siku hizi imepungua mno hivyo serikali imekataa kuziuza nje.",
"Asia\nBara la Asia lina nchi 44 na visiwa mbali mbali vya madola mbalimbali. Mlima mrefu kabisa ulimwenguni ambao ni mlima wa Everesti wenye urefu wa mita 8,850 (futi 29,035) ulioko Nepal pia uko kwenye bara hili. Kadhalika, nchi zenye wakazi wengi zaidi ulimwenguni China na India pia ziko kwenye bara hili."
] | 41
|
Je,makao makuu ya kaunti ya Samburu ni wapi?
|
[
"Kaunti ya Samburu\nMakao makuu yako Maralal."
] |
[
"Wasamburu\nWanaishi kaskazini ya ikweta katika kaunti ya Samburu, eneo la kilomita za mraba 21,000 (maili za mraba 8,000). Ardhi yao ni ya pekee na ni rembo. Kabla na miaka michache baada ya uhuru wa Kenya eneo hili lilikuwa linajulikana kama Northern Frontier District (NFD). Wilaya ya Samburu wakati moja ilikuwa sehemu kubwa ya NFD. Ni viongozi wa serikali tu ambao waliruhusiwa kuingia na ilikuwa imefungiwa kwa wageni wote wenye ukoo wa Kizungu na ukoo wa Kiafrika. Kibali maalumu kilichotolewa na utawala kilihitajika kuonyeshwa ili kuingia katika sehemu ya NFD. Hata leo sehemu hiyo bado ni eneo la mashambani. Kuna pia Hifadhi ya wanyama katika eneo hilo, Hifadhi ya Taifa ya Samburu.",
"Kaunti ya Samburu\nKaunti ya Samburu ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.",
"Kaunti ya Embu\nMto Tana hupitia katika kaunti hii, upande wa kusini na mashariki katika mpaka na kaunti za Machakos na Kitui. Sehemu hii ya Mto Tana huwa na malambo ya uzalishaji umememaji, yanayojulikana kama \"Seven Forks Dams\".Mbuga zilizo katika kaunti hiii ni sehemu ya Mbuga ya Kitaifa ya Mlima Kenya na Hifadhi ya Kitaifa ya Mwea inayopakana na Bwawa la Kamburu.",
"Kaunti ya Kiambu\nGavana, sasa Ferdinand Waititu, ndiye mkuu wa kaunti na serikali. Yeye huchaguliwa kwa muhula wa miaka mitano katika uchaguzi mkuu. Ana nguvu za utendaji na za kuteua wanakamati wa Kamati ya Utendaji ya Kaunti baada ya kuidhinishwa na Bunge la Kaunti. Hata ingawa mji mkuu wa kaunti uko Kiambu, utendaji wa serikali uko mji wa Thika.",
"Kiambu\nKiambu ni mji wa Kenya ya Kati, makao makuu ya kaunti ya Kiambu.",
"Wilaya ya Samburu\nMakao makuu yalikuwa mjini Maralal.",
"Mkoa wa Pwani (Kenya)\nPwani la Kenya ni nchi ya miji ya Waswahili hasa. Miji hii kama vile Lamu, Mombasa, Malindi, na mengi mengine iliyokuwa vituo vya biashara ya kimataifa tangu zaidi ya miaka 1000 iliyopita. Upepo wa monsuni ulibeba jahazi kutoka Uarabuni, Uajemi hata Bara Hindi kwenda pwani la Afrika ya Mashariki. Monsuni ulipogeuka kila baada ya nusu mwaka jahazi ziliweza kurudi kwao na bidhaa za biashara. Hivyo vituo vya biashara na mapunziko vikawa miji ya Waswahili, utamaduni uliounganisha tamaduni za wafanyabiashara Waarabu au Waajemi na Waafrika wenyeji wa pwani.",
"Kaunti ya Marsabit\nKaunti ya marsabit ni kavu. Ina Jangwa la Chalbi ambalo ni jangwa kweli la pekee katika Kenya. Kaunti za Marsabit, Turkana na Samburu hushiriki Ziwa Turkana. Mbuga ya Kitaifa ya Sibiloi hupatikana katika fuo za Ziwa Turkana katika upande wa Marsabit. Hifadhi ya Kitaifa ya Losai hupatikana katika mpaka wa Kaunti ya Marsabit na Samburu. Mlima Marsabit uko katika Hifadhi ya Kitaifa ya Marsabit. Mlima Kulal na Vilima vya Huri hupatikana katika kaunti hii.",
"Mto Kapai (Samburu)\nMto Kapai (Samburu) unapatikana katika kaunti ya Samburu, nchini Kenya (eneo la Bonde la Ufa la Afrika Mashariki)."
] | 15
|
Jina kamili la Pelé ni lipi?
|
[
"Pelé\n= Maisha ya awali =\nPelé alizaliwa mjini Três Corações, Minas Gerais, Brazil, na ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Fluminense Dondinho (mtoto wa João Ramos do Nascimento) na Celeste Arantes.Ni mkubwa kati ya watoto wawili. Alipewa jina la shujaa wa Kimarekani Thomas Edison. Wazazi wake waliamua kuitoa herufi \"i\" na kumuita \"Edson\",lakini kulikuwa na makosa kwenye cheti chake cha kuzaliwa kusababisha litumike jina la \"Edison\" badala ya \"Edson\".F amilia yake walimpa jina la \"Dico\". Alipewa jina la \"Pelé\" alipokuwa shule inaposemekana kuwa alishindwa kutamka jina la golikipa wa timu ya Vasco Da Gama anayeitwa Bilé,alivyozidi kulitamka ndivyo alivyozidi kuchapia. Pelé aliwahi kusema hakujua maana ya jina hilo wala marafiki zake waliompa jina hilo.Lakini jina hilo lilitokana na jina la Bilé lakini kwa Kiebrania maana yake ni maajabu (פֶּ֫לֶא),lakini jina halina maana yoyote kwa KIreno.",
"Pelé\nPelé (jina lake halisi ni Edison Arantes do Nascimento; amezaliwa 23 Oktoba 1940) alikuwa mchezaji wa mpira wa miguu kutoka Brazili. Anahesabiwa na wengi, kama waandishi wa habari na mashabiki, kuwa mchezaji mzuri zaidi wa wakati wote."
] |
[
"Pelé\nPelé alishinda taji kubwa kwa mara ya kwanza akiwa na Santos mwaka 1958 ambapo timu ailishinda taji la Campeonato Paulista; Pelé alimaliza mashindano akiwa mfungaji bora wa magoli 58, rekodi inayoshikiliwa hadi sasa.Mwaka mmoja baaadaye aliisaidia nchi yake kushinda mabao 3-0 dhidi ya Vasco Da Gama kwenye michuano ya Torneio Rio-São Paulo Santos hawakuwa na uwezo wa kushindana kwenye michuano hiyo.Mwaka 1960, Pelé alifunga magoli 33 akiisaidia timu yake kurudi tena kwenye michuano ya Campeonato Paulista na kubeba taji hilo lakini walifungwa kwenye michuano ya Rio-São Paulo baada ya kumaliza wakiwa nafasi ya nane.Kwenye msimu wa 1960, Pelé alifunga magoli 47 na kuisaidia Santos kubeba taji la Campeonato Paulista.Walisonga mbele na kubeba taji la Taça Brasil mwaka huohuo kwa kuwafunga Bahia kwenye fainali.Kwenye fainali,Pelé aliibuka mfungaji bora akiwa na magoli 9.",
"Pelé\nWakati msimu wa 1957 ulipoanza, Pelé alipewa nafasi katika kikosi cha kwanza akiwa na umri wa miaka 16 akawa mfungaji bora wa ligi.Miezi kumi baadaye aliitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Brazil.Baada ya kombe la dunia la 1958 na 1962,klabu tajiri za Ulaya kama Real Madrid, Juventus and Manchester United, walijaribu kutaka kumsajili.Mwaka 1958 Iner Milan walimsajili lakini Angelo Moratti ilimbidi akatishe mkataba huo baada ya mwenyekiti wa klabu ya Santos kushambuliwa na shabiki wa Kibrazili.Lakini mwaka 1961 serikali ya Brazil chini ya rais Jânio Quadros ilisema kuwa Pelé ni mchezaji kivutio kwa nchi hivyo haruhusiwi kuhamishwa kwenda nje ya nchi.",
"Pelé\nPelé alienda nchini Sweden akiwa na jeraha la goti lakini wenzake walimtetea ili aitwe kwenye kikosi.Mechi yake ya kwanza ilikuwa dhidi ya USSR kwenye mechi ya tatu kwenye mzunguko wa kwanza wa kombe la dunia la mwaka 1958,ambapo alimpa pasi Vavá iliyozaa goli la pili.Alikuwa mchezaji mdogo kuliko wote kwenye michuano na mchezaji mdogo kuwahi kucheza kombe la dunia.Dhidi ya Ufaransa kwenye nusu fainali,Brazili walikuwa wakiongoza 2-1.",
"Pelé\nPelé alikulia katika hali ya umaskini huko Bauru kwenye mji wa Paulo.Alijikusanyia fedha kidogo alipofanya kazi kwenye duka la chai.Alfundishwa kucheza mpira wa miguu na baba yake lakini hakuweza mara acheze na soksi iliyojazwa na magazeti au magada ya mapera huku akifunga na kamba.Amechezea klabu nyingi za vijana kama \"Sete de Setembro\", \"Canto do Rio\", \"São Paulinho\", na \"Amériquinha\". Pelé aliisaidia \"Bauru Athletic Club\" klabu ya vijana (ikifundishwa na Waldemar de Brito) kushinda mataji mawili ya mashindano ya klabu za vijana za São Paulo.Pelé alishindana mashindano ya mpira wa miguu ya ndani ya chumba ambapo aliisaidia timu yake ya Bauru.",
"Pelé\nPelé aliwahi kukiri kuwa mashindiano hayo yana changamoto kubwa,alisema kuwa kuwa mchezo huo ulikuwa wa haraka kidogo kuliko mpira wa miguu wa kwenye nyasi na kwamba mchezo huo ulihitaji uwezo mkubwa wa kufikiri haraka kwa kuwa kila watu wanakuwa karibukaribu ndani ya uwanja.Pelé anauheshimu sana mchezo huo kwa kuwa ulimpa uwezo mkubwa wa kufikiri papo kwa papo anapokuwa uwanjani.Licha ya hivyo mchezo huo ulimpa uwezo wa kuchezaccredits indoor football for helpin na wakubwa zaidi rika lake alipokuwa na umri wa miaka 14.Katika kila mashindano aliyowahi kucheza alikuwa akichukuliwa kama mdogo asingeweza kucheza lakini kila mashindano yanapoisha yeye ndiye anayekuwa mfungaji bora akiwa na magoli kumi na nne au kumi na tano.\"Hicho kilinipa kujiamini zaidi\", Pelé alisema\"Hapo nilijua kuwa nisiwe mwoga kwa chochote kile\".",
"Pelé\nMwaka 1956, de Brito alimpeleka Pelé Santos,mji wa viwanda na bandari karibu na São Paulo,alienda kwa majaribio kwenye klabu ya Santos FC,akiwaambia mabosi kuwa kijana wa miaka 15 atakuwa mchezaji mkubwa duniani.Pelé alimshangaza kocha Lula wakati majaribio kwenye uwanja wa Estádio Vila Belmiro, na akasaini mkataba na klabu hiyo Juni 1956.Pelé alitangazwa sana kwenye vyombo vya habari kuwa nyota wa baadae.Alianza vizuri Septemba 7 1956 akiwa na umri wa miaka 15 kwenye ushindi wa 7-1 dhidi ya Corinthians Santo Andre akishinda goli la kwanza.",
"Pelé\nPelé alianza kuichezea Santos akiwa na umri wa miaka 15 na timu ya taifa ya Brazil akiwa na miaka 16.Katika ngazi za kimataifa alishinda kombe la dunia mara tatu 1958,1962 na 1970,akiwa ni mchezaji wa pekee kufanya hivyo.Ni mchezaji wa kibrazili anayeongoza kwa magoli mengi zaidi kwa kufunga magoli 77 kwenye mechi 92.Kwenye ngazi ya klabu ni mfungaji bora wa muda wote katika klabu ya Santos, na aliisaidia kubeba taji la Copa Libertadores kwa miaka ya 1962 na 1963.Kwa mchezo wake wa haraka ,chenga zake na magoli yake ya ajabu yalimpa umaarufu duniani kote.Tangu alipostaafu mwaka 1977,Pelé amekuwa balozi wa mpira wa miguu duniani.",
"Soucis Ya Likinga\n\"Soucis Ya Likinga\" ni albamu iliyotoka mwaka 1986 kutoka kwa msanii wa muziki wa soukous kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Pepe Kalle. Albamu ina nyimbo nne tu, mbili upande A na mbili upande B. Hii ni albamu ya kwanza ya Pepe Kalle kuitengeneza akiwa nchini Ufaransa. Katika albamu Pepe Kalle katunga nyimbo mbili tu—Soucis Ya Likinga na Dadou 2e Version. Wakati Perfusion ukiwa utunzi wake Misha Mfum na Simplicité imetungwa na Solo Sita.",
"Ghana\nSoka ndiwo mchezo ulio na umaarufu zaidi nchini.\nTimu za kitaifa za soka ya wanaume zinajulikana kama The Black Stars, the Black Satellites na the Black Starlets na timu hizi hushiriki katika michuano mingi ikiwemo ile ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Kombe la Dunia la FIFA na Kombe la Dunia la FIFA kwa walio chini ya miaka 20. Timu ya the Black Satellites ilishinda Kombe la Dunia la FIFA kwa walio chini ya miaka 20 mnamo 2009 baada ya kushinda timu ya Brazili ya Seleção. Kuna timu za soka kadhaa nchini Ghana za kutajika zaidi zikiwa Accra Hearts ya Oak SC na Asante Kotoko baina ya zingine. Baadhi ya wachezaji wa soka wa Ghana wanaojulikana katika daraja ya kimataifa au waliopata ufanisi katika soka ya Ulaya ni Abedi Pele, Ibrahim Abdul Razak, Tony Yeboah, Anthony Annan, John Paintsil, Asamoah Gyan, Samuel Osei Kuffour, Richard Kingston, Sulley Muntari, Laryea Kingston, Stephen Appiah, Andre Ayew, Emmanuel Agyemang-Badu, Dominic Adiyiah na Michael Essien."
] | 38
|
Masinde muliro alijiunga na siasa mwaka gani?
|
[
"Masinde Muliro\nMwaka wa 1948, Muliro alijiunga na chama cha Kenya African Union (KAU), chama kilichoanzishwa kutetea maslahi ya Waafrika nchini Kenya ambayo wakati huo ilikuwa chini ya ukoloni.\nAlipoacha kufunza mwaka wa 1957, aligombea kiti cha ubunge cha eneo bunge la Nyanza Kaskazini ambacho wakati huo kilikuwa kinashikiliwa na W.W.W. Awori (kakake mkongwe wa makamu wa rais wa zamani wa Kenya, Moody Awori). Muliro alishinda uchaguzi.\nMiongoni mwa wabunge wenzake walikuwa Daniel Arap Moi ambaye aliyekuwa anawakilisha Bonde la Ufa, Tom Mboya ambaye aliyekuwa anawakilisha eneo la Nairobi, Bernard Mate ambaye aliyekuwa anawakilisha Mkoa wa Kati, Ronald Ngala ambaye aliyekuwa anawakilisha Mkoa wa Pwani, James Nzau Muimi ambaye aliyekuwa anawakilisha Mkoa wa Mashariki, Lawrence Oguda ambaye aliyekuwa anawakilisha Nyanza Kusini na Oginga Odinga ambaye aliyekuwa anawakilisha Nyanza ya Kati. Mwaka wa 1958 Muliro alianzisha chama cha Kenya National Party huku akiungwa mkono na wanachama 9 wa Legco(Legislative Council). Kisha alikibomia chama hicho na kujiunga na chama cha Kenya African Democratic Union (KADU). Hatimaye aliteuliwa kama Waziri wa Biashara kabla tu ya Kenya kupata uhuru mwaka wa 1963.\nMuliro alihudumu katika nyadhifa mbalimbali katika serikali za baadaye, lakini mara kwa mara alikuwa katika upande mbaya wa Rais Jomo Kenyatta. Baada ya kifo chake Kenyatta, Muliro alirejea Bungeni baada ya kushinda ombi mahakamani. Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Kitale Mashariki hadi mwaka wa 1988, wakati eneo bunge hili liligawanywa. Alishinda kiti kipya cha ubunge cha eneo bunge la Cherangany mwaka wa 1988, lakini alishikilia nyadhifa hiyo kwa muda wa miaka miwili tu. Katika uchaguzi wa wabunge wa mwaka wa 1990, kiti hicho cha Cherangany kilishindwa na Kipruto Arap Kirwa.",
"Masinde Muliro\nHenry Pius Masinde Muliro alizaliwa katika eneo la Kimilili nchini Kenya, mwana wa Muliro Kisingilie na mkewe Makinia. Wazazi wake walikufa wakati alipokuwa mchanga na alilelewa na kaka wa kambo, Aibu Naburuku.\nBaada ya masomo ya shule ya msingi na ya upili nchini Kenya na Uganda, alijiunga na Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini mwaka wa 1949. Alijiunga na kozi ya Shahada ya Sanaa katika Kiingereza, Historia na Falsafaya Siasa, na alihitimu mwaka wa 1953 akiwa na shahada za na Sanaa na Elimu. Mwaka wa 1954 alirejea nyumbani na mke wa asili ya Afrika Kusini, na alifundisha kwa muda katika shule ya serikali. Mwaka wa 1957, alipiga moyo konde kuiacha kazi hiyo ya ualimu na kujiunga na siasa."
] |
[
"Masinde Muliro\nMasinde muliro (alizaliwa mnamo 1922 na aliaga dunia mnamo 14 Agosti 1992) alikuwa mwanasiasa wa Kenya, mmoja wa viongozi wakuu katika kuchagiza siasa nchini Kenya. Alikuwa mpigania uhuru aliyejulikana na alifanya kampeni kwa ajili ya marejesho ya demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya katika miaka yake ya mwisho.\nAlikuwa muhawiliki asiye na mzaha wala huruma na mtu wa amani aliyejihusisha sana kwa siasa. Mmoja wa wanasiasa safi zaidi katika historia ya Kenya , rekodi ambayo inaweza pinzaniwa tu na Musikari Kombo na Ronald Ngala.\nAlikuwa anajulikana kama mmoja wa viongozi bora ambao kamwe hawakuwahi kuwa rais, na kama hangeupa dunia mkono wa buriani, nafasi zilikuwa kwamba angemshinda Daniel Arap Moi kwa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 1992.",
"Elijah Masinde\nMara ya kwanza kabisa kufungwa ilikuwa ni mwaka 1945. Serikali ya kikoloni ilishindwa kumwelewa Masinde na kuamua kumchukilia kama mwendawazimu na hivyo kumweka katika hospitali ya vichaa ya Mathare kwa maiaka miwili. Mwaka 1948 Masinde alishtakiwa kwa kosa la uhaini na kupelekwa uhamishoni huko Lamu ambako alikaa hadi mwaka 1961. Baada ya kuachiliwa huru, Masinde aliendelea na shughuli za kidini na kisiasa. Alikuwa akiunga mkono chama cha Kenya African National Union (KANU) jambo ambalo lilimpunguzia umaarufu wake kwakuwa watu wengi wa eneo analotoka walikuwa wakiunga mkono chama cha Kenya African Democratic Union (KANU).",
"Moïse Katumbi\nMnamo 29 Septemba 2015 alijiuzulu kuwa Gavana, baada ya viongozi wa vyama saba vya siasa walipofurushwa kutoka kwenye Upande wa Wengi wa Urais kwa kuandika barua kwa Kabila ambapo waliuliza nia yake ya kujiondoa mwisho wa muhula wake wa pili mwaka wa 2016. Katumbi aliongeza kuwa kujiuzulu kwake kutoka kwenye People's Party for Reconstruction and Democracy kungalimruhusu kuangazia majaribio ya serikali ya taifa kukiuka katiba na kuchelewesha uchaguzi na pia kupata uhuru wake wa kuongea na kuchukua hatua. Katika azimio lilo hilo, alitangaza kuwa ushauri muhimu miongoni mwa wanachama wa mashirika ya raia ungalifanyika ili kuunda vuguvugu la jamhuri na demokrasia nchini. Mnamo 19 Desemba 2015, Moïse Katumbi alijiunga na watu wengine mashuhuri wa Kongo katika muungano ulioitwa \"Front Citoyen 2016\". Chombo hiki kinajishughulisha na kulinda Katiba na kuhakikisha kuwa uchaguzi wa mwaka wa 2016 unafanyika.",
"David Mathayo David\nMwanzo wa siasa\nSiasa alizianza rasmi mwaka 1995 alitumia TV yake kwenda kuonyesha vijijini madhara ya vyama vingi, alitumia mapigano ya Rwanda na Burundi kama kutishia wananchi wasikubali upinzani na kipindi kile wananchi walikuwa wepesi kuelewa kumbuka TV hazikuwa nyingi Tanzania kipindi kile. Alijijengea umaarufu sana ndani ya chama mkoani Morogoro na kitaifa. Aligombea ujumbe wa NEC mkoa wa Morogoro kundi la vijana alishinda. Mathayo alimaliza SUA 1997 na kupata kazi ya kufundisha chuo kimoja huko Serowe Botswana. Kwa kuwa mjumbe wa NEC alikuwa karibu na akina Lowasa, JK na vingunge wengine aliweza kuwa anaonana na akina Makamba na akawa ni mwanamtandao. Wakati huo Matayo alikuwa akirudi Tanzania kufanya shughuli zake za kisiasa wakati bado ni mwajiriwa wa serikali ya Botswana. Kwa mfano wakati mmoja alirudi Tanzania na kuwahamasisha wanafunzi wa SUA (kama 200 hivi) na kuwapeleka Dodoma kupokea kadi za CCM chini ya mwenyekiti wa CCM Mkapa. Wanafunzi walahidiwa wangepatiwa ajira kwa kufanya hivyo. Hii ilimjenga sana Matayo ambaye aliisha kuwa maarufu kwenye ofisi za chama Dodoma, kama mjumbe wa NEC na mkutano mkuu. Mwaka 2000 aligombea Ubunge Same Magharibi na kushinda na kuteuliwa kuwa waziri mdogo. Wakti huu aliisha tamka kwamba amesomea Afrika Kusini digrii ya falsafa (PhD). Prof Msolla wakati aliyekuwa waziri wa elimu ya juu na sayansi ambaye aliwahi kufundisha SUA alimjua sana Matayo na alimwita Matayo na kumuuliza kuwa PhD alifanya lini na wapi na pia aletee PhD thesis yake. Prof Msolla alisema \"Matayo aliogopa sana na alikili mbele yangu, kuwa Prof mimi nimetumia hii title kisiasa zaidi, sina MSc wala PhD”.",
"Halima James Mdee\nAlipata ajira katika Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana mwaka 2004 akiwa Ofisa Maendeleo kama mwanasheria mpaka mwaka 2005 alipoamua kuacha kazi na kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, ambako alishiriki kuwapigia kampeni wagombea mbalimbali wa CHADEMA kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa viti maalumu.",
"Ushairi wa Christopher Richard Mwashinga\nKama miezi saba tangu alipojiunga na kundi hili la Matadi SDA, idara ya vijana ya kundi iliandaa tamasha la vijana kama sehemu ya programu maalumu za kufungia mwaka. Hapo ndipo kiongozi wa vijana wakati huo, Bw. Yohana Jackson, alipomwomba Christopher Mwashinga aandike shairi litakaloimbwa wakati wa tamasha hilo, naye akakubali. Kwa hiyo siku ya Ijumaa, Desemba 27, 1985 Christopher Mwashinga, wakati huo akiwa na umri wa miaka ishirini, alitunga shairi la beti nane aliloliita,”Tunapomaliza Mwaka.” Shairi hili liliimbwa kesho yake, Jumamosi Desemba 28, 1985 wakati wa tamasha lililofana sana la vijana wa kundi hilo. Hilo ndilo lililokuwa shairi lake la kwanza alilotunga lenye maudhui ya kidini. Ubeti wa saba wa shairi hilo una maneno yafwatayo:",
"Michael Wamalwa Kijana\nKuingia kwake siasa nchini Kenya kulikuja katika uchaguzi wa ubunge wa 1974. Akiwa tu na umri wa miaka 30, wapinzani wake walimpuzilia yeye kama kijana na pia kutoka familia ya kitajiri mno ili kuwakilisha eneo bunge lake vyema. Kampeni yake ilikuwa ya kifahari: ilijumuisha matumizi ya ndege na mikutano ya kampeni za umma iliyoja ufujaji wa pesa. Hatimaye alishinda kiti cha mwaka 1979, kwa kushirikiana na Masinde Muliro.",
"Masinde Muliro\nMwaka wa 1989, Muliro aliungana na Kenneth Matiba, Charles Rubia, Martin Shikuku, Phillip Gachoka na Oginga Odinga kuunda FORD (Forum for Restoration of Democracy), ni kundi shinikizo lililotaka kurejeshwa kwa siasa ya vyama vingi. Baada ya mapigano ya vurugu kati ya wafuasi wa FORD polisi na wafuasi wa serikali na polisi, serikali ya KANU lilikubali siasa ya vyama vingi mwaka wa 1991. FORD ikawa chama huku Muliro akiwa Makamu wa Mwenyekiti."
] | 29
|
Kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement ni nani?
|
[
"Kenya\nKatika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 27 Desemba 2007, Rais Kibaki wa chama cha Party of National Unity (PNU) aliwania uchaguzi dhidi ya chama kikuu cha upinzani Orange Democratic Movement (ODM). Kulingana na wachunguzi wa kimataifa, uchaguzi huo ulikumbwa na udanganyifu na hivyo kutofikia kiwango kinachokubalika kimataifa. Chama cha ODM kilisambaratika na kupoteza 8 % ya kura zake kwa chama kipya cha Orange Democratic Movement-Kenya (ODM) - kikiongozwa na Kalonzo Musyoka. Kinyang’anyiro kilikuwa kikali kati ya mgombea wa ODM, Raila Odinga na Kibaki wa PNU. Kuhesabiwa kwa kura na Tume ya Uchaguzi ya Kenya kulionyesha Raila akiongoza kwa kura chache na baadaye kwa kura nyingi. Hata hivyo, kura zilipoendelea kuhesabiwa na Tume ya Uchaguzi, Kibaki alimkaribia mpinzani wake kwa kura, kisha akamshinda. Matokeo hayo yalisababisha maandamano na kulaumiwa kwa Tume ya Uchaguzi ya Kenya kwa kumpendelea Kibaki,hivyo Oginga akajitangaza “rais wa watu” na kutaka kura zihesabiwe tena.",
"Orange Democratic Movement\nKufuatia umoja wao katika kura ya maoni na mjadala wa kukabiliana na tisho kutoka kwa chama kipya cha NARC-Kenya, viongozi wa KANU, LDP na baadhi ya vyama vidogo waliamua kuungana hadi kwa uchaguzi mkuu ujao wa 2007 ,na kutengeneza chama cha Orange Democratic Movement, ambalo jina lake lilitokana na alama ya chungwa iliyowakilisha kutokubaliana \"No\" katika kura ya maoni ya katiba. Hata hivyo, wakili Mugambi Imanyara aliweza kusajili ODM kama chama kabla ya muungano , na kulazimisha wao kutumia bendera ODM-Kenya.",
"Orange Democratic Movement\nKatika mwaka wa 2007 muungano huu ulianza kutokuwa imara, ambapo makundi mengine yalijiondoa. Chama cha Uhuru Kenyatta KANU ndicho kwanza, kujiondoa mwezi wa Julai mwaka wa 2007 na kuunga kuchaguliwa tena kwa Rais Kibaki , ingawa baadhi ya wanasiasa binafsi kutoka KANU walibaki katika ODM. kutokana nakutoelewana kati ya Kalonzo Musyoka na Raila Odinga, chama cha ODM kiligawanyika katika makundi mawili katika katikati mwa mwezi wa August2007.. Kundi la Raila, ambayo pia ni pamoja naMusalia Mudavadi, William Ruto, Joseph Nyagah na Najib Balala walijiondoa kayika ODM Kenya kuchukua chama cha ODM ambacho kilisajiliwa na Mugambi Imanyara, wakati huo kundi la Kalonzo, likiongozwa na yeye mwenyewe na Dr Julia Ojiambo llibakia katika asili ODM - Kenya.",
"Orange Democratic Movement\nMakundi mawili yalifanya uchaguzi wamgombea urais siku mfululizo katika jumba la michezo Kasarani mjini Nairobi. Tarehe 31 Agosti 2007, Kalonzo Musyoka alishinda Julia Ojiambo ili kuwaania urais na tiketi ya ODM-Kenya,na tarehe 1 Septemba Raila Odinga alishinda Ruto, Mudavadi, Balala na Nyagah. Kulikuwa na madai kuwa baadhi ya wajumbe walihudhuria na kupiga kura katika uteuzi wa pande zote na kusababisha tatizo la uanachama wa vyama nchini Kenya. Raila na Kalonzo kisha walikabiliana na rais Kibaki katika uchaguzi mkuu. Kibaki alitangazwa kama mshindi wa uchaguzi katika mazingira ambayo yalikuwa yalifafanuliwa kama \"questionable\" kwa waangalizi mbalimbali. Raila Odinga na wafuasi wake hawakukubali matokeo gombana, na hii yalisababisha mgogoro vurugu kuenea nchini kote, kwa ujumla aidha kati ya wafuasi wa chama.",
"National Rainbow Coalition\nNational Rainbow Coalition (NARC) ni chama cha kisiasa nchini Kenya kilichoanzishwa kabla ya uchaguzi wa mwaka 2002.\nIlikuwa muungano wa vyama mbalimbali vya upinzani dhidi ya KANU na rais Daniel arap Moi. Ilikuwa hasa na pande mbili:\nMsingi wa ushirikiano ulikuwa mapatano kati ya pande za NARC yaliyoitwa \"Memorandum of Understanding\" (MoU). Hapo walipatana ya kuwa:\nNARC ikashinda uchaguzi wa 2002 na Kibaki akawa rais mpya. LDP ilikuwa na wabunge wengi kati ya vyama vya NARC. Lakini Kibaki hakutekeleza azimio la pamoja katika \"Memorandum of Understanding\" kupatia LDP nusu ya mawaziri wala kuwezesha mabadiliko ya katiba ya kumpa Odinga nafasi ya waziri mkuu.\nLDP iliendelea kudai mapatano yafuatwe, ikakataliwa na polepole kuelekea upande wa upinzani hata kama bado ilikuwa sehemu ya serikali.\nKatika miaka iliyofuata farakano ilikua. Mwaka 2005 Kibaki alijaribu kupitisha katiba mpya isiyopunguza sana mamlaka za afisi ya rais. Hapa sehemu kubwa ya LDP pamoja na KANU wakiungana kwa harakati ya machungwa (ODM) walipinga pendekezo la katiba katika kura maalumu ya wananchi, na pendekezo likakataliwa na wananchi.\nKibaki alijibu kwa kufuta serikali akiwaachisha mawaziri wote. Serikali mpya ilikuwa bila wawakilishi wa LDP tena.\nSasa Raila pamoja na Uhuru wa KANU waliunda harakati mpya ya ODM (Orange Democratic Movement) kwa kusudi la kugombea uchaguzi wa 2007.\nHii ilikuwa mwisho wa NARC kama chama tawala.\nKiongozi wa kisheria alikuwa Charity Ngilu asiyekubaliwa na sehemu ya viongozi waliokuwa karibu na rais. Hivyo walianzisha 2006 kitengo kipya kwa jina la NARC-Kenya iliyoingia 2007 katika maungano ya PNU ya Kibaki. \nNgilu aliamua Septemba 2007 kusimama upande wa Raila Odinga. Katika uchaguzi wa 2007 NARC iliweza kusimamisha wagombea wachache nje ya maungano ya Orange Democratic Movement na watatu walichaguliwa.",
"Orange Democratic Movement\nODM ilianzishwa na chama cha Uhuru Kenyatta, KANU na chama cha Raila Odinga, LDP, lakini chama cha KANU kiliweza kujiondoa, na waliobaki waligawanyika katika makundi haya mawili yanayoongozwa na Raila Odinga (ODM; ndio wengi zaidi) na Kalonzo Musyoka (ODM-Kenya). Sababu ya farakano ilikuwa suala la nani atakuwa mgombea wa urais upande wa ODM.",
"Wiper Democratic Movement\nMakundi hayo mawili yalifanya uchaguzi wa kumchagua mgombea wao wa urais siku kadhaa mfululizo katika jumba la michezo la Kasarani mjini Nairobi. Tarehe 31 Agosti 2007, Kalonzo Musyoka alimshinda Julia Ojiambo kwa tiketi ya ODM-Kenya. Tarehe 1 Septemba, Raila Odinga alichaguliwa mgombea urais wa ODM. Raila na Kalonzo walikabiliana na rais Kibaki katika uchaguzi mkuu. Kalonzo aliibuka wa tatu, lakini mnamo Januari 2008, akawa makamu wa rais wa Kenya chini ya Kibaki, ambaye ushindi wake ulikataliwa na Raila Odinga na ODM.",
"Orange Democratic Movement\nKufuatia kupitishwa kwa sheria ya vyama vya siasa. Chama cha ODM, kilifanya uchaguzi wa ndani yake mwishoni mwa Desemba 2008 pamoja na Waziri Mkuu Raila Odinga anayeibukia kama kiongozi wa chama, na Waziri wa viwanda Henry Kosgey kama mwenyekiti wa chama. Hata hivyo kutokana na fadhaa juu ya kikanda na uwakilishi wa jinsia, baadhi ya vyeo vya chama viliundwa si kuhiyo."
] |
[
"Orange Democratic Movement\nKura ya kutokubaliana'No' ambayo chama cha ODM kilifanyia kiampeni ilishida kwa asilimia 58.12%ya Wakenya waliopiga kura na kuweka chini katiba iliyopendekezwa, na kupatia Chungwa ushindi. Baada ya katiba kukataliwa Rais Mwai Kibaki aliwaodoa mawaziri. Wanachanma wa ODM walisema kwamba hii ilikuwa ni hatua katika mwelekeo sahihi, lakini kukawa na wito wa haraka wa uchaguzi mkuu katika serikali nzima Kenya, wakidai kuwa serikali ya Kibaki imepoteza mamlaka yake kwa sababu ya matokeo ya kura ya maoni ambayo serkali hii iliunga mkono. Serkali ya Kibaki ilipinga uchaguzi huu na haukufanyika mpaka wiki ya mwisho ya miaka mitano ya mamlaka aliyopewa Kibaki. Hata hivyo, ODM imeibuka kama chama cha upinzani mkubwa pamoja na KANU, imepanga mikutano kadhaa ya kampeni kota nchini ikidai uchaguzi na katiba mpya miongoni mwa madai mengine. Pia,chama cha ODM kilipinga mawaziri wapya wa rais Kibaki. Chama chaLiberal Democratic Party (LDP), ambacho kilipinga katiba mpya, kilishushwa nje ya mawaziri.",
"Uhuru Kenyatta\nKatika kura maalumu ya wananchi kuhusu katiba Uhuru alishikamana na viongozi wa LDP katika kambi ya Chungwa. Mipango yake ya kushiriki katika Orange Democratic Movement (ODM) yalipingwa vikali ndani ya chama kwa sababu wanaKANU pamoja na rais mstaafu Moi waliogopa kupotea kwa chama cha kwanza katika historia ya Kenya.",
"Orange Democratic Movement\nOrange Democratic Movement (ODM) (jina kamili: Orange Democratic Movement Party of Kenya ni chama cha kisiasa nchini Kenya. Kilianzishwa mwaka 2006 katika maandalizi ya uchaguzi wa bunge la Kenya wa mwaka 2007, lakini asili yake ni harakati za kura juu ya katiba mpya nchini Kenya ambayo ilianzishwa mwaka 2005 kwa ajili ya kura ya maoni ya katiba ya Kenya.",
"Orange Democratic Movement\nKatika uchaguzi wa rais Raila Odinga alitangazwa kuwa ameshindwa na rais Kibaki kwa kura 230,000. Lakini watazamaji wengi waliona kasoro katika hesabu ya kura na ODM ilidai kuwa Odinga ni mshindi halali. ODM ilifaulu vizuri upande wa viti vya bunge la Kenya. Ilipata karibu nusu ya wabunge wote yaani 99 kati ya 120 ikawa kubwa katika bunge baada ya uchaguzi wa Desemba 2007 na 99 wajumbe wa bunge na akaenda mbele kwa kushinda 3 nje ya tano kwa-uchaguzi mapema mwaka 2008. Hata hivyo inaonekana kwamba hali ya kupoteza Wabunge bado imekabili chama hili ambapo kumekuwana uchaguzi mara mbili katika majimbo ya wabunge ambao ODM wawili waliuawa katika mwanzo wa mwaka zaidi kuliko wabunge wawili walikufa baada ya kuanguka na ndege."
] | 0
|
Ngugi wa Thiong'o alizaliwa wapi?
|
[
"Ngugi wa Thiongo\nNgugi amezaliwa Kenya katika kijiji cha Kamiriithu karibu na Limuru, wilaya ya Kiambu katika jamii ya Wagikuyu akabatizwa James Ngugi. Alikuwa mtoto wa tano wa mke wa tatu wa baba yake Thiong'o wa Nducu. Baba alikuwa mkulima aliyepotea shamba lake kutokana na Waingereza kuteka na kutwaa Nyanda za Juu za Kenya. James alisoma shule za wamisionari za Kamaandura (Limuru), Karinga (Mangu) na Alliance High School (Kikuyu). Katika miaka ile akawa Mkristo. Wakati alikisoma shule familia yake iliathiriwa na vita ya Maumau ikawa kaka yake aliuawa na mama yake aliteswa."
] |
[
"Ngugi wa Thiongo\nKazi yake ya kifasihi ilimpeleka katika mzozo na serikali. Kuanzia mwaka 1976 Ngugi alishirikiana na wanakijiji Wagikuyu karibu na Limuru kuanzisha maagizo ya tamthilia katika lugha yao. 1976 riwaya yake ya \"PETALS OF BLOOD\" ilichora picha ya watawala wapya Waafrika jinsi walivyochukua nafasi ya wakoloni wa awali wakidharau na kukandamiza wananchi. Mwaka uleule aliandika tamthilia ya \"Ngaahika Ndeenda\" (Nitaolewa nitakapopenda). Wakubwa katika serikali walikuwa na wasiwasi wakiogopa mwelekeo wa kimarxist wa Ngugi hasa alipotoka katika Chuo Kikuu na kuingia kati ya wananchi wa kawaida kwa njia ya maigizo yake katika lugha ya Gikuyu. Makamu wa Rais wa Kenya Moi aliamua kumkamata Ngugi kwa misingi ya sheria ya usalama wa kitaifa wakati Rais Jomo Kenyatta mwenyewe tayari alikuwa amedhoofika kutokana na uzee na ugonjwa.",
"Ngugi wa Thiongo\nNgũgĩ wa Thiong'o (amezaliwa 5 Januari 1938) ni mwandishi Mkenya aliyeandika kwa Kiingereza lakini siku hizi anatumia lugha ya Gikuyu.",
"Ngugi wa Thiongo\n1973 alirudi Nairobi kama Profesa wa Kiingereza na mwenyekiti wa idara ya fasihi. Idara hii ilianzishwa kutokana na upinzani wa Ngugi na wenzake dhidi ya hali ya Kiingereza kuwa nguzo kuu ya elimu katika Afrika. Katika makala 'On the Abolition of the English Department' aliyoandika 1968 pamoja na Taban lo Liyong na Henry Owuor-Anyumba, aliwahi kuuliza \"Tukihitaji kutazama historia ya utamaduni mmoja kwa undani kwa ajili ya masomo yetu, kwa nini tusichague utamaduni mmoja wa Kiafrika na kuupa kipaumbele ili tulinganishe tamaduni mbalimbali nao?\" Kutokana na msimamo huo aliendelea kutafiti fasihi ya simulizi ya makabila ya Kenya, hasa ya Wagikuyu na fasihi ya Kiswahili.",
"Kikuyu (lugha)\nTangu zamani za koloni Gikuyu imewahi kuandikwa. Vitabu vya kwanza kwa Gikuyu vilikuwa Biblia na vitabu vya ibada. Tangu uhuru waandishi mbalimbali walianza kuandika. Anayejulikana zaidi ni Ngugi wa Thiong'o na kati ya riwaya zake iko \"Mũrogi wa Kagogo\". Waandishi wengine ni Mwangi wa Mutahi na Gatua wa Mbugwa.",
"Francis Imbuga\nHatima ya jamii ya Waafrika ilyozungukwa na itikadi ngeni ndio ilokuwa dhamira na maudhui ya kazi za waandishi waanzilishi wa Afrika,kazi ambazo Imbuga alizisoma.Kazi za Ngugi wa Thiong'o kama vile Weep Not, Child (1964), The River Between (1965), na The Black Hermit (1968) zina maudhui makuu ya mabadiliko ya kihistoria ya Waafrika na mizozo inayotokana na kuwepo kwa Wazungu katika Afrika.. Imbuga alizisoma kazi hizi pamoja na za waandishi wengine kama vile Elvania Zirimu, Peter Nazareth, Jonathan Kariara,na Okot p'Bitek.",
"Kenya\nNgugi wa Thiong'o ni mmoja wa waandishi maarufu wa Kenya. Kitabu chake, \"\" ni ufafanuzi wa maisha yalivyokuwa Waingereza walipoitwaa Kenya. Hii ni hadithi kuhusu athari za Mau Mau katika maisha ya Wakenya weusi. Kinavyochanganya maudhui - ukoloni, elimu, na mapenzi - kunakifanya kuwa kimojawapo kati ya vitabu bora vya hadithi barani Afrika.",
"John Ngugi\nNgugi ni mzaliwa wa Kigumo na mafanikio yake ya mapema ya kimataifa yalikuja katika michuano ya dunia Cross Country, ambapo alishinda taji nne mfululizo kati ya mwaka wa 1986 na 1989 (hii ililkuwa rekodi ya uanariadha) na kwa ujumla taji tano.",
"John Ngugi\nJohn Ngugi Kamau (alizaliwa mnamo 10 Mei 1962 katika sehemu ya Kigumo, wilayani Muranga) [8] ni mkimbimbiaji wa zamani wa Kenya na mara nyingi huitwa mmoja wa wanariadha bora nchini katika mbio za “cross-country” na ni mshindi wa mita 5,000 katika Olimpiki ya mwaka wa 1988.",
"John Ngugi\nNgugi alijiimarisha mwenyewe kama mkimbiaji wa mburuzo yake aliposhinda mbio ya mita 5000 katika Michuano ya Dunia ya mwaka wa 1987 katika mji mkuu wa Roma. Katika fainali, Ngugi alichukua uongozi alipofikia kilomita ya pili, lakini licha ya mbinu zake za uongozi katika mbio hizo, alipitwa na wanariadha wenzake wakati wa kumaliza, na kumaliza katika nafasi kumi na mbili; nafasi ya kusikitisha. Alishinda mbio za mita 5000 katika Michezo ya All-Africa ya mwaka wa 1987 uliofanyika nchini Kenya."
] | 35
|
Je,Steven Zuber alijiunga na klabu ya Hoffenheim mwaka upi?
|
[
"Steven Zuber\nMnamo Agosti 14 mwaka 2014, Zuber alihamia Hoffenheim juu ya mkataba wa miaka minne. Mnamo 25 Januari 2017, aliongeza mkataba wake hadi 2020."
] |
[
"Steven Zuber\nSteven Zuber (alizaliwa tarehe 17 Agosti mwaka 1991) ni mchezaji wa soka wa Uswisi ambaye anacheza kama kiungo wa klabu ya Ujerumani Hoffenheim na timu ya taifa ya Uswisi.",
"Steven Zuber\nZuber alifanya timu yake ya kwanza kwa tarehe 12 Julai 2008 katika Kombe la Intertoto , mechi ya pili ya mguu dhidi ya KS Besa, ambako alikuja kama mbadala wa dakika ya 83. Mnamo Agosti 3, alifanya sura yake ya kwanza ya Uswisi Super League katika safu ya 1-1 na Vaduz.",
"Makoto Hasebe\nIliripotiwa mwezi wa 10 2007 atajiunga na klabu iitwayo A.C Siena katika ligi ya Itali eti timu hiyo imeweza kuchukua saini yake na atajiunga na klabu hiyo Januari, lakini haikuwa sahihi, maana baadae alijiunga na klabu ya Vfl Wolfsburg na alikuwa mchezaji wa kwanza kabisa kutoka Japan kuichezea klabu hiyo ya Vfl Wolfsburg na alikuwa ni mchezaji wa pili kutoka Japan kuchukuwa ubingwa wa Bundesliga baada ya mchezaji aitwaeYasuhiko Ukudera",
"Roberto Firmino\nFirmino iliyosainiwa na Hoffenheim mnamo Desemba 2010, na mkataba uliendelea mpaka Juni 2015. Aliwasili rasmi huko Hoffenheim tarehe 1 Januari 2011. Kisha meneja wa Hoffenheim Ernst Tanner alisema kuwa \"walifurahi kuajiri mchezaji wa Brazil mwenye uwezo mkubwa\". Firmino aliipatia Hoffenheim mafanikio makubwa.",
"Sibusiso Zuma\nZuma ilianza wasifi wake katika klabu za Afrika Kusini kama vile Mighty Pa, African Wanderers na Orlando Pirates. Mwezi Juni mwaka wa 2000, alijiunga na klabu ya Kideni ya FC København, ambapo alijiendeleza kama mchezaji. Aliisaidia klabu yake kushinda taji la ligi ya Kideni kwa mara yake ya pili na aliteuliwa kuingia katika “hall of fame” ya klabu kutokana na jitihada zake bora katika msimu wa 2004-05, na mwaka wa 2001 Zuma aliteuliwa katika nafasi ya 29 katika tuzo la mwanakandanda bora wa FIFA wa mwaka wa 2001. Baada ya miaka 5 ½ katika klabu ya FC København, Sibusiso Zuma aliuzwa kwa klabu ya Bundesliga, ambayo ni ya ligi ya Kijerumani, Arminia Bielefeld kwa kitita cha yuro milioni moja mnamo Julai 2005.",
"André Schürrle\nAlianza kazi yake mnamo tarehe 05 mwaka 2009, akitumia miaka miwili kwenye klabu kabla ya uhamisho wa £ 6.5 milioni kwa Bayer 04 Leverkusen. Maonyesho yake huko alipata kipaumbele cha Chelsea, ambaye walimsajili kwa mkopo wa milioni 18 mwaka 2013. Schürrle alicheza msimu wa Ligi Kuu ya Ligi Kuu ya Uingereza kabla ya kujiunga na VfL Wolfsburg kwa £ 22 milioni Januari 2015, kushinda DFB-Pokal na DFL-Supercup katika mwaka wake wa kwanza.",
"Mohamed Zidan\nAlishiriki na klabu hiyo katika mechi 10 na alifunga magoli 2,baadaye klabu hiyo ikamwuza kwa njia yakuazima katika klabu ya Ujerumani nyingine inayoitwa 1. FSV Mainz 05 kunzia mwaka 2005 hadi 2006. Katika klabu hiyo alifunga magoli 10 katika mechi 30 na alionekana kuwa mchezaji mzuri tena alipendwa na washabiki wa timu hiyo hadi walitamani abaki ila haikuwezekana kwani Werder Bremen ikamuomba arudie kutokana na uchezaji wake mzuri ulionekana katika klabu hiyo ya Mainz.",
"Wojciech Szczęsny\nBaada ya kuanza kazi yake katika klabu ya Legia Warsaw, Szczęsny alijiunga na Arsenal mwaka 2006. Baada ya mwaka mmoja alihamia Brentford kwa mkopo msimu uliofuata, baadaye akawa golikipa bora katika klabu yake, alishinda makombe mawili ya FA na kuwa mpokeaji wa Golden Glove ya 2013-14 pamoja na mwenzake Petr Čech.",
"Antonio Valencia\nMwanzoni mwa msimu uliyofuata, alijiunga na klabu ya Ligi ya Uingereza, Wigan Athletic, awali kama mpango wa mkopo kwa muda wa mwaka moja. Alicheza mechi yake ya kwanza ya Wigan tarehe 19 Agosti 2006, mechi ambayo Wigan ilipoteza 2-1 dhidi ya Newcastle United, na aliifungia Wigan bao lake la kwanza dhidi ya Manchester City tarehe 21 Oktoba 2006. Muda wa mkopo uliongezwa hadi msimu uliyofuata, na tarehe 18 Januari 2008 alihamia Wigan rasmi kwa kitita cha ada ambacho hakikutangazwa, na alisaini mkataba wa miaka tatu unusu. Alikataa kuihamia timu ya La Liga ya Real Madrid mnamo Januari 2009. Mapema juni mwaka wa 2009, mwenyekiti wa Wigan alitangaza kuwa hatamlazimisha Valencia kubaki katika klabu.",
"Steven Zuber\nMnamo tarehe 5 Julai 2013, Zuber alisaini mkataba wa miaka mitano na mabingwa wa Ligi Kuu ya Urusi ya CSKA Moscow. Alianza tarehe 13 Julai dhidi ya Zenit St Petersburg katika Kombe la Urusi la mwaka 2013, ambalo CSKA alishinda 3-0."
] | 32
|
Dodoma iko na idadi ngapi ya watu?
|
[
"Mkoa wa Dodoma\nKatika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa Mkoa wa Dodoma ilihesabiwa kuwa 2,083,588.",
"Dodoma (mji)\nEneo la mji liko mita 1135 juu ya usawa wa bahari UB. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, mji wa Dodoma ulikuwa na wakazi wapatao 410,956 waishio humo."
] |
[
"Dodoma vijijini\nDodoma Vijijini ilikuwa wilaya moja ya Mkoa wa Dodoma wenye msimbo wa posta 41200. Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa Wilaya ya Dodoma Vijijini ilihesabiwa kuwa 440,565 .",
"Mkoa wa Dodoma\nKwa jumla Dodoma haina mvua nyingi isipokuwa sehemu za wilaya za Mpwapwa na Kondoa. Hivyo hasa mazao yasiyotegemea sana mvua hulimwa kama vile mtama, wimbi, muhogo; kilimo cha mahindi hupatikana mara kwa mara na matatizo ya kukosa mvua. Mazao ya sokoni ni karanga alizeti na simsim. Dodoma ni pia mwanzo wa ustawishaji wa mizabibu na uzalishaji wa divai katika Tanzania.",
"Kiwanja cha Ndege (Dodoma)\nKiwanja cha Ndege ni jina la kata ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma , Tanzania yenye msimbo wa posta 41115. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 10129 waishio humo.",
"Viwandani (Dodoma)\nViwandani ni jina la kata ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma , Tanzania yenye msimbo wa posta 41102. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 4883 waishio humo.",
"Mkoa wa Bagamoyo (DOA)\nLakini tangu kuanzishwa kwa reli ya kati kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro (1907), halafu hadi Dodoma mwaka 1910 na hadi Tabora mwaka 1912 biashara ya misafara ilizidi kupungua pamoja na idadi ya watu walioishi Bagamoyo na mnamo mwaka 1913 walikuwa 5,000 tu.",
"Kikuyu Kaskazini\nKikuyu Kaskazini ni jina la kata ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma , Tanzania yenye msimbo wa posta 41111. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 9852 waishio humo.",
"Kilimani (Dodoma)\nKilimani ni jina la kata ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma , Tanzania yenye msimbo wa posta 41110. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 6471 waishio humo.",
"Mkoa wa Dodoma\nKutokana na hali ya hewa mifugo ni mingi (ng'ombe 1,600,000, mbuzi 954,000, kondoo 274,000, nguruwe 23,000, kuku takriban 1,400,000). Idadi ya mifugo imeongeza tatizo la mmomonyoko wa ardhi katika sehemu za mkoa.",
"Kizota\nKizota ni jina la kata ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma , Tanzania yenye msimbo wa posta 41114. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 34453 waishio humo.",
"Iyumbu (Dodoma mjini)\nIyumbu ni jina la kata ya Dodoma Mjini katika Mkoa wa Dodoma , Tanzania. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 2700 waishio humo."
] | 13
|
Je,mtoto wa umri wa miaka mbili anaweza pata ugonjwa wa kisukari?
|
[
"Maziwa ya mama\nKunyonyesha kunaendelea kutoa manufaa katika na baada ya kipindi cha utoto. Faida hizi ni pamoja na kupunguzwa kwa dari hatari ya kifo cha ghafla kwa watoto wachanga (SIDS), inaongeza akili, inapunguza uwezekano wa kuambukizwa ugonjwa wa katikati mwa sikio, homa, na viini vinavyolete homa, hupunguza uwezekanno wa kupata baadhi ya saratani kama vile sarateni ya damu kwa watoto lukemia, kupunguza hatari ya mwanzo wa ugonjwa wa kisukari wa mtoto, hupunguza hatari ya pumu na ezema, hupunguza matatizo ya meno, Hupunguza hatari ya fetma baadaye katika maisha, na hupunguza uwezekano wa kupata matatizo ya kisaikolojia."
] |
[
"Draft: Chanjo ya matumbwitumwi\nChanjo ya matumbwitumwi inazuia ugonjwa wa matubwitumwi. Watu wengi wakichanjwa huwa inapunguza matatizo ndani ya jamii. Inafaa zaidi kama asilimia 90% ya wananchi wakichanjwa na ubora wake unakadiriwa kuwa asilimia 85% ya wananchi. Dozi mbili zinahitajika ili kukinga ugonjwa huo kwa muda mrefu. Dozi ya kwanza inapendekezwa kwa watoto wenye miezi 12 hadi miezi 18. Dozi ya pili kwa kawaida watoto wanapewa wakiwa wana miaka miwili hadi sita. Kwa watoto ambao hawajachanjwa akiugua anaweza kupewa dozi kinga.",
"Kanisa la Kiorthodoksi la Eritrea\nNdoa huweza kuanzishwa au kupangwa wakati mwanamume ana umri wa miaka kumi na..., au ishirini na... Kiutamaduni, wasichana wanaruhusiwa kuolewa wakiwa na umri wa miaka 14 hadi 18, lakini katika karne ya 20, mambo yamebadilika, hivyo sasa umri mdogo kuliko wote wa kuolewa ni miaka 18, na suala hili linasimamiwa na serikali. Ndoa za kiserikali ni nyingi japo pia, wapo watu wanaofunga ndoa katika makani mbalimbali. Na baada ya kufunga ndoa kanisani, suala la talaka halipo na haliwezekani. Kila familia hufanya sherehe ya ndoa baada ya harusi.",
"Kanisa la Kiorthodoksi la Ethiopia\nNdoa huweza kuanzishwa au kupangwa wakati mwanamume ana umri wa miaka kumi na..., au ishirini na... Kiutamaduni, wasichana wanaruhusiwa kuolewa wakiwa na umri wa miaka 14 hadi 18, lakini katika karne ya 20, mambo yamebadilika, hivyo sasa umri mdogo kuliko wote wa kuolewa ni miaka 18, na suala hili linasimamiwa na serikali. Ndoa za kiserikali ni nyingi japo pia, wapo watu wanaofunga ndoa katika makani mbalimbali. Na baada ya kufunga ndoa kanisani, suala la talaka halipo na haliwezekani. Kila familia hufanya sherehe ya ndoa baada ya harusi.",
"Uzazi wa mpango kwa njia asilia\nKwa kuzingatia tabia hizo mbili tofauti, maharusi wakitaka mtoto wa kiume wanatakiwa kufanya tendo la ndoa siku ya kwanza baada ya kilele (kujisikia kuteleza) na kuendelea kwa miandamo 6 ya hedhi.\nKama mwanamke hajapata mimba baada ya miandamo 6, waanze kuonana siku ya kilele na siku inayofuata. Kama mwanamke amekosa siku ya kilele, yaani kama utelezi wa ute unaendelea siku inayofuata, waonane tena siku inayofuata.",
"Maradhi ya zinaa\nChunguzi zinaonyesha kuwa wenye umri kati ya miaka 16 na 24 wapo katika hatari kubwa zaidi ya kupata magonjwa ya zinaa kuliko watu wa makamo kwa sababu vijana wanaweza kuwa na wenzi wengi wa mapenzi kuliko kuwa na mahusiano ya muda mrefu na mwenzi mmoja. Zaidi, vijana wanaweza wakaona ugumu kuwaambia wenzi wao kuwa wameambukizwa magonjwa ya zinaa. Vijana pia wanaweza kuona aibu au kutokuwa na uwezo wa kutafuta matibabu ya magonjwa haya. Hii inamaamisha si tu kuwa wanaweza kuambukiza ugonjwa kwa vijana wenzao bali pia wana hatari kubwa ya kupata madhara yanayosababishwa na kutotibu ugonjwa kwa muda mrefu.",
"Kisukari aina ya 2\nAina ya 2 ya kisukari kwa kawaida ni ugonjwa sugu unaohusiana na upungufu wa matarajio ya kuishi kiasi cha miaka kumi Kwa upande mmoja, jambo hili husababishwa na matatizo yanayohusiana na kisukari ikiwa ni pamoja na: hatari ya mara mbili hadi nne ya ugonjwa wa moyo na mishipa ikijumuisha ugonjwa wa moyo wenye iskemia na kiharusi, ongezeko la hadi mara 20 la kiwango cha kukatwa miguu na ongezeko la kulazwa hospitalini.. Katika nchi zilizostawi, na sehemu zingine kwa viwango vinavyoongezeka, ugonjwa wa kisukari aina ya 2 ndio kisababishi kikuu zaidi cha upofu usiotokana na majeraha na matatizo ya figo. Ugonjwa huu pia umehusishwa na ongezeko la hatari ya matatizo ya kiutambuzi na dimenshia kupitia kwa taratibu za magonjwa kama vile Ugonjwa wa Alzeheimer na dimenshia ya mishipa. Matatizo mengine ni pamoja na: akanthosi nigrikani, uhanithi na maambukizi ya kila mara.",
"Ulemavu\nUlemavu wa kiakili unatokea kwa viwango tofauti sana. Mara nyingi hautambuliki hadi mtoto anapoingia shule na huko anachelewa kujifunza. Hata hapo ni lazima kutofautisha kama tatizo ni ulemavu wa akili au ulemavu wa kujifunza tu. Wengine wanaishia kiwango cha elimu kinacholingana na uwezo wa mtoto wa wastani mwenye miaka 9-12 na wanaweza kujifunza kazi inayowawezesha kudumisha maisha yao wakiwa watu wazima.",
"Upara\nMatukio ya upara wa kiolezo hutofautiana miongoni mwa idadi kubwa ya watu kwa misingi ya maumbile ya jeni; sababu za kimazingira hazionekani kuathiri sana aina hii ya upara. Utafiti mmoja mkubwa uliofanywa katika Maryborough, Victoria, Australia ulionyesha kuwa kiwango cha ya upotezaji nywele za mbeleni mwa kichwa-katikati hulingana na ongezeko la umri na huathiri 73.5% ya wanaume na 57% ya wanawake wenye umri wa miaka 80 na zaidi. Kwa mujibu wa tovuti ya Medem Medical Library, upara wa kiume huathiri takribani wanaume milioni 4 nchini Marekani. Takriban asilimia 25 ya wanaume huanza kupata upara tokea umri wa miaka 20, theluthi mbili huanza kupata upara kuanzia miaka 60. Uwezekano wa kupata jeni ya upara ni 4 kwa 7.",
"Ukuaji wa binadamu\nAnahitaji kutiwa moyo (anapenda ukweli na sifa) ajihisi anaweza kufanya kitu, atambue mahitaji ya wengine na kuwasaidia wayapate. \nUmri wa miaka 13-20 ni kipindi cha mpito chenye mabadiliko mengi yanayoathiri mwendo mzima wa kijana ili atoke utoto na kuingia utu uzima. Msichana anabalehe mapema kuliko mvulana. Mvulana ana mwamko mkubwa kuliko msichana. Kuna mvuto mkubwa kati yao, hivyo wanahitaji kuongozwa na nidhamu safi (maadili ya unyago). Ni kipindi cha [[vurugu na cha [[hisi kali]] (kulia, kucheka n.k.). [[Akili]] inapanuka sana na kupenda [[nadharia]]; hivyo ni wakati wa kujipatia [[maarifa]].",
"Skizofrenia\nWatu walio na umri wa takriban miaka 18 na walio katika mwanzo wa utu uzima wako katika kiwango cha juu zaidi cha kupata skizofrenia. Miaka hii ni muhimu katika kuendelea kijamii na kitaaluma katika maisha ya vijana. Katika asilimia 40 ya wanaume na asilimia 23 ya wanawake wanaotambuliwa na skizofrenia, hali hii hujionyesha kabla ya umri wa miaka 19. Ili kupunguza matatizo ya ukuaji yanayohusishwa na skizofrenia, hivi karibuni juhudi nyingi zimefanyika ili kutambua na kutibu awamu ya ugonjwa inayotokea kabla ya dalili kuanza. Awamu hii ya “kabla ya mwanzo” imeshatambuliwa hata miezi 30 kabla ya dalili kuanza.Wakati wa awamu ya kabla ya mwanzo, watu ambao hupata skizofrenia baadaye wanaweza kuwa na dalili za muda mrefu au zilizo na kikomo au dalili kuu sanapamoja na dalili zisizo maalum za kujitenga na watu, hasira na hisia za kijumla za kukosa furaha pakubwa na kuzembea ."
] | 33
|
Je,Flamingo inapatikana katika ziwa gani nchini Kenya?
|
[
"Utalii nchini Kenya\nMbuga ya wanyama ya kitaifa ya Ziwa Nakuru, lililoanzishwa mwaka wa 1961 karibu na Ziwa Nakuru, liko karibu na mji wa Nakuru. Inajulikana sana kwa maelfu, na wakati mwingine mamilioni ya ndege wa aina ya flamingo wanaokusanyika ufuoni mwa ziwa Nakuru. Wajihi wa ukame wa ziwa hili ni vigumu kujulikana kwa sababu ya flamingo wengi. Idadi ya flamingo katika ziwa hutegemea maji na hali ya chakula. Pahali bora kuwatazama ndege hawa ni juu ya mwinuko unaoitwa \"Baboon Cliff\".",
"Ziwa Natron\nHili ndilo ziwa pekee katika eneo la Afrika Mashariki ambalo kwa kawaida flamingo milioni 2.5 ambao ni wadogo na ambao huhofiwa maisha yao hufugwa. Kiwango cha chumvi kiongezekapo, cyanobacteria pia huongekeka, na ziwa yaweza kusaidia viota zaidi. Flamingo hao, kundi kubwa zaidi katika Afrika Mashariki, hukusanyika pamoja katika maziwa ya chumvi, ambapo hujilisha Spirulina (mwani ya rangi ya buluu na kijani na pigmenti nyekundu). Ziwa Natron ni sehemu salama kufuga Flamingo wale wadogo kwa sababu mazingira yake ni kikwazo dhidi ya wanyama wanaokula wenzao wanaojaribu kufikia viota vyao. Flamingo wakuu pia hufuga katika sehemu zenye ardhi zilizonyooka.",
"Ziwa Magadi (Kenya)\nZiwa Magadi lipo kusini mwa Kenya katika mkoa wa Bonde la Ufa, kaskazini mashariki mwa Ziwa Eyasi. Wakati wa kiangazi 80% ya ziwa hili huwa limejaa Sodium kabonati na ni maarufu kwa aina mbali mbali za ndege zinazoishi kando kando ya ziwa hilo kwa mfano flamingo."
] |
[
"Jangwa\nMto wa Ewaso Nyiro katika Kenya ya kaskazini kwa kawaida hukwisha katika nchi yabisi za Usamburu. Lakini kila baada ya miaka makumi kadhaa baada ya mvua kubwa sana inaendelea kuvuka jangwa la Somalia ya kusini na kufikia Bahari Hindi jinsi ilvyotokea wakati wa El-Nino 1998.",
"Mto Gandeni\nMto Gandeni unapatikana katika kaunti ya Mombasa, kusini mashariki mwa Kenya (kwenye bahari ya Hindi).",
"Mto Kadingo\nMto Kadingo unapatikana katika kaunti ya Kwale, kusini mashariki mwa Kenya (kwenye bahari ya Hindi).",
"Mto Logogo\nMaji yake yanaishia katika ziwa la magadi linaloitwa Turkana na lililo kubwa kuliko maziwa yote ya Kenya. Ni pia ziwa la jangwani lililo kubwa kuliko yote duniani.",
"Mto Gandi (Kilifi)\nMto Gandi (Kilifi) unapatikana katika kaunti ya Kilifi, kusini mashariki mwa Kenya (eneo la pwani).",
"Mto Kai-Ekongo\nMaji yake yanaishia katika ziwa la magadi linaloitwa Turkana na lililo kubwa kuliko maziwa yote ya Kenya. Ni pia ziwa la jangwani lililo kubwa kuliko yote duniani.",
"Mto Vigurungani\nMto Vigurungani unapatikana katika kaunti ya Kwale, kusini mashariki mwa Kenya (kwenye bahari ya Hindi).",
"Ziwa Nakuru\nZiwa Nakuru ni mojawapo ya maziwa ya magadi katika Bonde la Ufa. Linapatikana kusini mwa mji wa Nakuru, katika eneo la kati nchini Kenya na linazungukwa na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Nakuru. Hifadhi hiyo ilianzishwa mwaka 1961. Ilianza ndogo, ikizingira ziwa hilo maarufu na maeneo ya milima yaliyo karibu. Na sasa imeongezwa kujumuisha sehemu kubwa ya maeneo ya mbuga."
] | 15
|
Je,Raila Odinga alikuwa waziri mkuu mwaka upi?
|
[
"Raila Odinga\nRaila Amolo Odinga (*7 Januari 1945) ni mwanasiasa wa upinzani nchini Kenya na tangu 13 Aprili 2008 waziri mkuu nchini humo hadi 2013. Aliwahi kuwa mbunge tangu 1992 na waziri katika serikali ya rais Mwai Kibaki kati ya 2001 hadi 2005. Katika uchaguzi wa mwaka 2007 alikuwa mgombea wa urais upande wa Orange Democratic Movement (ODM). Ajulikana kote Kenya kwa jina la la kwanza Raila. Waluo wenzake hupenda kumwita \"Agwambo\"."
] |
[
"Raila Odinga\nAlizaliwa 1945 katika familia ya Waluo akiwa mtoto wa chifu Jaramogi Oginga Odinga aliyekuwa makamu wa rais wa kwanza nchini Kenya. Baba yake alikuwa kiongozi mkuu wa Waluo akatazamiwa baadaye kama mpinzani mkuu wa rais wa kwanza Jomo Kenyatta. \nKaka yake Raila, Oburu Odinga amekuwa mwanasiasa na mbunge vilevile.",
"Raila Odinga\nKatika miaka iliyofuata farakano ilikua. Mwaka 2005 upande wa rais Kibaki ulijaribu kuanzisha katiba mpya usiokuwa na mabadiliko mengi kuhusu madaraka ya rais. Cheo kipya cha waziri mkuu kikapangwa kuwa na madaraka machache. Vilevile ugatuzi wa madaraka hayakuonekana jinsi ilivyowahi kukubaliwa katika mkutano wa Bomas of Kenya. Katiba hii ilitakiwa kukubaliwa na wananchi wote. Kempeni ya kura hii ikagawa taifa hata mawaziri wa serikali walionekana pande zote mbili. Watetezi wa katiba iliyopendekezwa walitumia ishara ya ndizi na wapinzani walitumia ishara ya chungwa. Raila pamoja na chama cha KANU kilichokuwa chama cha upinzani tangu 2002 wakafaulu kuzuia katiba katika kura ya wananchi wote. Kibaki akajibu kwa kuachisha mawaziri wote pamoja na Raila na kutomwita tena katika serikali mpya.",
"Raila Odinga\nUchaguzi mwenyewe ulikuwa na matatizo kwa sababu matokeo ya kwanza yalimwonyesha Raila kuwa na kura nyingi lakini Tume la Uchaguzi lilisimamisha matangazo ya matokeo ghafla. Matangazo yaliyofuata baada ya siku mbili ghafla yalimwonyesha Rais Kibaki kuwa na kura nyingi akaapishwa haraka bila kusubiri muda wa kisheria kwa malalamiko. Odinga alitangazwa na ODM kama mshindi wa kweli na farakano hili lilisababisha ghasia kali sana zilizoendelea kukaribia hali ya vita ya wenyewe kwa wenyewe. Watu wengi walifukuzwa katika maeneo hasa ya Bonde la Ufa na pia katika mitaa ya vibanda kwenye miji mbalimbali kufuatana na kabila yao. Baada ya vifo ya watu maelfu na kuporomoka kwa uchumi nchini majadiliano kati ya pande zote mbili chini ya Kofi Annan yalileta maelewano juu ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa na Kibaki kama rais na Raila kama waziri mkuu.",
"Orange Democratic Movement\nMakundi mawili yalifanya uchaguzi wamgombea urais siku mfululizo katika jumba la michezo Kasarani mjini Nairobi. Tarehe 31 Agosti 2007, Kalonzo Musyoka alishinda Julia Ojiambo ili kuwaania urais na tiketi ya ODM-Kenya,na tarehe 1 Septemba Raila Odinga alishinda Ruto, Mudavadi, Balala na Nyagah. Kulikuwa na madai kuwa baadhi ya wajumbe walihudhuria na kupiga kura katika uteuzi wa pande zote na kusababisha tatizo la uanachama wa vyama nchini Kenya. Raila na Kalonzo kisha walikabiliana na rais Kibaki katika uchaguzi mkuu. Kibaki alitangazwa kama mshindi wa uchaguzi katika mazingira ambayo yalikuwa yalifafanuliwa kama \"questionable\" kwa waangalizi mbalimbali. Raila Odinga na wafuasi wake hawakukubali matokeo gombana, na hii yalisababisha mgogoro vurugu kuenea nchini kote, kwa ujumla aidha kati ya wafuasi wa chama.",
"Raila Odinga\nNARC ikashinda uchaguzi na Kibaki akawa rais mpya. Raila akaingia katika serikali kama waziri wa barabara. Lakini Kibaki hakutimiza MoU. LDP haikupata nusu ya mawaziri. Mkutano wa kusahihisha katiba ulikwamishwa na na mapendekezo ya mkutano wa kutunga katiba mpya katika Bomas of Kenya hayakutekelezwa. Cheo cha waziri mkuu haukuanzishwa.",
"William Ruto\nKatika Januari mwaka wa 2006, Ruto alitangaza hadharani kwamba atawania kuwa rais katika uchaguzi mkuu ujao, uliopangwa kufanyika mwezi wa Desemba 2007. Taarifa yake alisstumiwa na baadhi ya wanachama wa KANU wake, pamoja na rais wa zamani Daniel arap Moi. Ruto alitaka uteuzi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) kama mgombea wa urais wake, lakini katika kura cha chama mnamo tarehe moja Septemba 2007, yeye alikuwa wa tatu kwa kura 368, nyuma ya mshindi, Raila Odinga (kwa kura 2,656) na Musalia Mudavadi (na 391). Ruto aliuunga mkono Odinga baada ya kura. Yeye alijiuzulu kutoka wadhifa wake kama katibu mkuu wa KANU tarehe 6 Oktoba 2007.",
"Nana Akufo-Addo\nMwishoni mwa utawala wa kijeshi wa Jerry Rawlings alianza tena kuandaa chama kipya cha NPP kuanzia mwaka 1992. \nKuanzia mwaka 1996 hadi 2008 alichaguliwa mara tatu kuwa mbunge. Mwaka 1998 alijaribu kuwa mgombea wa urais kwa niaba ya chama cha NPP lakini hakufaulu. Aliendelea kumfanyia kampeni mgombea mshindi John Kufuor. Baina ya 2001 na 2007 alikuwa waziri katika serikali ya rais huyo, kwanza kama waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu, halafu kama Waziri wa Mambo ya Nje ya Ghana.",
"Kenya\nTarehe 12 Februari 2008 Kibaki na Odinga walitia sahihi mkataba wa kuunda serikali ya muungano ambapo Odinga angekuwa waziri mkuu wa pili nchini Kenya. Kulingana na mkataba huo, rais angeteua baraza la mawaziri kutoka pande zote mbili za PNU na ODM kulingana na wingi wa wabunge wa kila chama bungeni. Mkataba huo ulieleza kuwa baraza la mawaziri litajumuisha Makamu wa Rais na manaibu wawili wa Waziri Mkuu. Baada ya majadiliano bungeni ilipitishwa kuwa muungano huo utadumu hadi mwisho wa kipindi cha bunge, ama chama kimoja kikijitoa kwenye muungano kabla ya kipindi cha bunge kuisha.",
"Raila Odinga\nKatika uchaguzi wa 1997 alimaliza nafasi ya tatu kaa mgombea wa rais baada ya Moi na Mwai Kibaki. Akaingia katika bunge kati ya vyama vya upinzani lakini akaanza kujenga maelewano na Moi na chama cha KANU. Wapinzani wake Raila walisema ya kwamba shabaha zake za kiuchumi zilikuwa sababu muhimu katika badiliko wakidai ya kwamba biashara za Raila zilisogea mbele wakati ule wa ushirioano na Moi. Watetezi wake walisema ya kwamba aliona upinzani ulikuwa umegawnyika mno akaona njia ya pekee ya kubadilisha hali ya nchi ilikuwa ushirikiano na KANU."
] | 0
|
Mji mkuu wa Nigeria ni?
|
[
"Mji mkuu\nNigeria iliamua mwaka 1976 kuhamisha mji mkuu wa kitaifa kutoka Lagos kwenda mahali pa katikati ya nchi. \"Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho\" limeteuliwa. Mji mpya wa Abuja ndani ya eneo hili ukawa mji mkuu wa Nigeria mwaka 1991.",
"Abuja\nAbuja ni mji mkuu wa Nigeria. Idadi ya wakazi wake imekadiriwa kuwa watu 178,462 . Mwaka wa 1976, serikali ya Nigeria iliamua kuanzisha mji mkuu mpya badala ya Lagos. Wakachagua katikati ya nchi, na mipango ya ujenzi ikaundwa chini ya makampuni matatu ya Marekani: PRC Corporation; Wallace, McHarg, Roberts na Todd; na Archisystems. Mipango hiyo ikabadilishwa baadaye na Kenzo Tange, msanifu majengo maarufu wa Japani. Abuja ikatangazwa rasmi kuwa mji mkuu wa Nigeria tarehe 12 Desemba 1991. Iko mahali pa 9, 10, Kaskazini na 7, 10, Mashariki.",
"Nigeria\nMji mkuu ni Abuja ikitanguliwa na Lagos hadi mwaka 1991."
] |
[
"Enugu\nHapo wali Enugu ilikuwa mji mkuu wa Mkoa wa Mashariki wakati Nigeria ilipata uhuru mwaka wa 1960. Tarehe 27 Mei 1967, serikali ya Nigeria iligawanya mikoa hii tatu katika majimbo 12. Mkoa wa Mashariki ulivunjwa na Enugu ilifanywa mji mkuu wa Jimbo Kuu ya Mashariki. Tarehe 30 Mei 1967, ilitangazwa kama mji mkuu wa taifa ya wa Jamhuri ya Biafra; tarehe 28 Septemba 1967, wakati Enugu ilitekwa na askari wa Nigeria,mji mkuu wa Biafran ulihamia Umuahia.\nMwishonim wa Vita vya Nigeria mwaka wa 1970, Enugu tena ikawa mji mkuu wa Jimbo Kuu ya Mashariki. Tarehe 3 Februari 1976, Jimbo Kuu Mashariki lilivunjwa katika majimbo mawili mapyaAnambra naIMO{/ 0} . Enugu ikawa mji mkuu wa jimbo laAnambra.\nMwaka wa 1991, udikteta wa kijeshi wa Ibrahim Babangida uligawanya jimbo la Anambra katika majimbo mawili mapya, jimbo la Enugu na jimbo la Anambra . Enugu alibakia kama mji mkuu wa jimbo lipya la Enugu, wakati huoAwka ikawa mji mkuu wa Anambra .\nWazawa kuu ya mji huu ni Ogui Nike ambao wanaishi katika maeneo yanayozunguka Hotel Rais na Obiagu na Ama-Igbo maeneo, kama vile Onu-Ihewuzi na maeneo ya Asata. Vikundi vingine ni pamoja na watu wa Awkunanaw , ambao wanaishi hasa katika eneo la Achara na maeneo ya Uwani;watu wa Enugwu Ngwo , ambao wanaishi juu ya vilima na mashamba yao yameenea kote bonde. Ugunduzi wa makaa ya mawe katika ardhi yao ilisababisha kuongezeka kwa makazi katika viini vya milima na wakazi walivyoongezeka, mji ulipanika katika maeneo mengine. Mji huu uliitwa Enugwu Ngwo kabla ya kubadilishwa na kuitwa Enugu . Wakazi wa Nike hasa huishi katika Abakpa, Iji-Nike, na Emene maeneo ya mji mkuu wa jimbo.",
"Niamey\nNiamey ni mji mkuu wa Niger. Iko mwambaoni wa mto Niger. Ikiwa na wakazi 674,950 (sensa ya 2002) Niamey ni mji mkubwa wa Niger na kitovu cha kiutawala, kiuchumi na kiutamaduni.",
"Siasa ya Nigeria\nShirikisho limegawanywa katika majimbo 36 na eneo 1 *; makao mkuu ya shirikiho (Abuja) *, Abia, Adamawa, Akwa Ibom, Anambra, Bauchi, Bayelsa, Benue, Borno, Cross River, Delta, Ebonyi, Edo, Ekiti, Enugu, Gombe, IMO, Jigawa, Kaduna, Kano, Katsina, Kebbi, Kogi, Kwara, Lagos, Nasarawa, Niger, Ogun, Ondo, Osun, Oyo, Plateau, Rivers, Sokoto, Taraba, yobe, Zamfara\nKila jimbo limegawanywa katika Maeneo ya Serikali za Mitaa yanayojilikana kwa luga ya kimombo kama LGAs. Kuna LGAs 774 nchini Nigeria. Maeneo haya yameorodheshwa katika makala kwa kuwa jimbo. Jimbo la Kano lina idadi kubwa ya Serikali za Mitaa kwa mitaa 44, na Bayelsa ndilio jumba amabalo lina kiasi ambayo ni 9 . Mji mkuu wa shirikisho hili Abuja ina mitaa 6 . Maeneo ya Serikali za Mitaa yalichukua nafasi ya Wilaya ambayo ilikuwa kitengo cha tatu chini wakati wa utawala wa serikali ya Uingereza.",
"Ahmadu Bello\nKatika uchaguzi wa kwanza uliofanyika Kaskazini mwa Nigeria mwaka 1952, Bwana Ahmadu Bello alishinda [[kiti[[ cha bunge cha Kaskazini, na kuwa mwanachama wa [[baraza tendaji]] kikanda kama [[waziri wa kazi]]. Bello aliweza kufanikiwa kuwa [[waziri wa Ujenzi]], katika Serikali za Mitaa, na ya [[Ustawi wa Jamii]] katika Mkoa wa Kaskazini mwa Nigeria.\nMwaka wa [[1954]], Bello aliweza kuwa [[mkuu]] wa kwanza wa Kaskazini mwa Nigeria. Katika Uchaguzi mkuu huru wa mwaka wa [[1959]], Bello aliongoza NPC kushinda viti vingi vya [[bunge]]. Chama cha Bello NPC kiliungana na chama cha [[Nnamdi Azikiwe]] NCNC [[(Baraza la Taifa la Nigeria na Kamerun)]] na kuunda serikali ya kwanza ya shirikisho la Nigeria ambayo ilileta [[uhuru]] kutoka Uingereza. Katika kutengeneza shirikisho la serikali huru ya Nigeria mwaka wa [[1960]], Bello alichagua kubaki mkuu wa Kaskazini mwa Nigeria na kumwachia [[makamu wa rais]] wa NPC [[Abubakar Tafawa Balewa]] nafasi ya [[Waziri Mkuu]] wa [[Shirikisho]] hilo.\nTendo kuu la Bello na urithi mkubwa alioacha ni kuunganisha watu mbalimbali wa Kaskazini mwa Nigeria. Aliuawa wakati wa [[mapinduzi ya kijeshi]] baada ya kuangusha serikali huru nchini Nigeria tarehe 15 Januari 1966 alipokuwa anatumikia kama mkuu wa Kaskazini mwa Nigeria wakati huo.",
"Jimbo la Niger\nJimbo la Niger ni jimbo upande wa magharibi mwa nci ya Nigeria na ndilo jimbo kubwa nchini humo. Mji mkuu wake ni Minna na miji mikubwa mingine ni Bida, Kontagora na Suleja. Liliundwa mwaka wa 1976 wakati Jimbo la Kaskazini Magharibi liligawanywa na kuunda majimbo ya Sokoto na Niger.",
"Siasa ya Cote d'Ivoire\nMji mkuu rasmi tangu 1983 ni Yamoussoukro; hata hivyo, Abidjan unabaki kuwa kitovu cha utawala. Nchi nyingi huweka balozi zao mjini Abidjan, ijapokuwa baadhi yao (ikiwa ni pamoja na Uingereza) wamefunga harakati zao kwa sababu ya fujo zinaoendelea na ushambuliaji dhidi ya Wazungu. Wakazi wanaendelea kupata shida kwa kufuatia vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea.",
"Jimbo la Ebonyi\nJimbo la Ebonyi ni jimbo la nchi kavu lililoko kusini-mashariki mwa Nigeria, kimsingi, wakaazi wake ni Waigbo (95% ya idadi ya watu). Mji mkuu wake na mji mkubwa ni Abakaliki. Afikpo ni mji mkubwa wa pili. Miji mikubwa mingine ni Edda, Onueke, Nkalagu, Uburu, Onicha, Ishiagu, Amasiri na Okposi. Ni mojawapo ya majimbo sita mpya nchini Nigeria yaliyoumbwa mwaka wa 1996;Ebonyi aliumbwa kutoka kwa tarafa ya zamani ya Abakaliki ya Jimbo la Enugu na tarafa ya zamani ya Afikpo ya Jimbo la Abia.",
"Siasa ya Nigeria\nRais huchaguliwa na watu. Yeye ni mkuu wa nchi na kiongozi wa serikali na pia mkuu wa Shirikisho Mtendaji wa Baraza. Nigeria ina mzunguko wa urais ili kanda kuu tatu za Nigeria (Kaskazini, Mashariki na Magharibi) kushiriki kudhibiti siasa ya nchi.\nTawi mtendaji imegawanywa katika Wizara zifuatazo:"
] | 26
|
Je,nani mwanzilishi wa mziki wa hIhop nchini Tanzania?
|
[
"Machozi Jasho na Damu\nHalkadhalika ame-enzi kazi ya mwanzilishi halisi wa rap ya Kiswahili nchini Tanzania bwana Edward Mtui (maarufu kama Fresh XE) kwa kuchukua kiitikio chake cha \"Piga Makofi\" ambacho kilimpelekea ashinde tuzo ya Yo Rap Bonanza katika miaka ya 1980, lakini hakutoa nyimbo. Jay anatungia wimbo kiitikio hicho na ndani yake anataja wale wote walioifikisha hip hop ya Tanzania hapa kwa kuwataja.",
"Bongo Flava\nMwanzilishi wa hip hop ya Tanzania ni Mr. II (pia anajulikana kama Sugu au 2-Proud), ambaye alitoa kibao chake cha kwanza maarufu cha Bongo flava, \"Ni Mimi\" mnamo 1995. Mr. II bado yupo hadi leo (rekodi yake ya mwisho ni \"Coming of Age\", ilitolewa mnamo 2007). Kundi la kwanza la hip hop la Tanzania, Kwanza Unit, 1993. Awali walikuwa wanaimba kwa Kiingereza lakini hatimaye wakawa wanaimba kwa Kiswahili. Moja kati ya wanachama wa zamani wa kundi hili ni Professor Jay, kwa ni moja kati ya wasanii maarufu wa hip hop nchini Tanzania. Vilevile kundi la Diplomate lililokuwa na kina Saigon."
] |
[
"Nash MC\nAlipitia mengi yanayohitajika ili kuwa mchanaji hasa. Alipata msaada kutoka kwa wasanii wakongwe wa hip hop ya Tanzania kama akina Lindu Lindulu, Zavara Mponjika, Saigon na wengine wengi tu. Kwenye mwaka wa 2009 alifanya mahojiano ya nguvu na Saigon wakati huo mtangazaji katika kipindi cha \"HIP-HOP Base\" cha EATV. Mahojiano haya Nash aliongea mengi ya msingi kuhusu uwanja wa hip-hop na alivyorudi katika kuchana alikuwa tofauti na zamani kabisa. Baadaye akaja kutoa \"Nani Mkali Kwenye Game\" chini ya mtayarishaji Kita ndani Ramo Records huko Magomeni, Dar es Salaam. Hiyo ilikuwa mwaka 2010. Mwaka 2011 anatoa kandamseto ya kwanza \"Hazina Sura ya Kwanza\" halafu akaendelea kutoa albamu kila mwaka uliofuata hadi 2014. Mwaka wa 2012 \"Mzimu wa Shaaban Robert\", mwaka wa 2013 \"Chizi\", mwaka wa 2014 Mchochezi. Albamu zote zimetazamia maisha halisi ya raia wa Tanzania na Afrika kwa ujumla jinsi wanavyopitia magumu yao ya kila siku.",
"Hoyce Temu\nPamoja na kuendeleza sanaa ya urembo nchini Tanzania, ni mtangazaji wa kipindi cha runinga \"Mimi na Tanzania\"\nalichokianzisha mwaka 2011 kikiwa na lengo la kuyaibua matatizo ya watu wenye uhitaji ili waweze kupata msaada (fedha, faraja au fedha na faraja); mpaka tarehe 18 Mmachi 2016 kipindi hicho kimeweza kusaidia watu 1,000 na bado kinaendelea kusaidia watu zaidi.",
"Hussein Mkiety\nSharo ndiye msanii wa kwanza wa vichekesho nchini Tanzania kufanya ucheshi bila kuvaa midabwada. Awali ilionekana kawaida sana kwa mchekeshaji kuvaa midabwada ili aonekane anachekesha. Au kuvaa nguo zenye mwonekano wa kipekee tofauti na hali ya kawaida. Hili alionesha mapinduzi ya hali ya juu. Baadaye alikuja kushiriki katika filamu ya Chumo iliyoongozwa na Jordan River yenye maudhui ya kupambana na ugonjwa wa malaria. Vilevile amepata kuonekana katika video ya \"Sababu ya Ulofa\" ya Top C. Alifamika sana kwa staili yake ya \"Ooh mama\" ambayo ndiyo ilikuja kuwa kama alama ya kumtambulisha Sharo katika kila kazi. Vilevile alikuwa na uhusiano wa karibu na King Majuto, ambaye walishiriki ote katika filamu ya Alosto. \nMnamo tarehe 26 Novemba, 2012 ni siku ambayo alipata ajali hukohuko Tanga akiwa sio mbali sana na nyumbani kwa mama yake ambako alikuwa anaenda kusamlimu. Ajali ilitokea saa mbili usiku, huku ikitipotiwa kuwa mwendokasi ndiyo kiini cha ajali hiyo. Hussein alikuwa anaenda Tanga kwa mama yake kumpatia fedha kwa ajili kulimia shamba na baadaye aanze ujenzi wa nyumba imara kwa ajili ya mama yake mzazi. Alikuwa anaendesha gari aina ya Toyota Harrier. Kifo kiligubikwa na dhana nyingi za ushirikina, huku marafiki wa karibu (Kitale) wakiweweseka juu ya kuondoka mapema duniani kwa Sharo.",
"Washirika Tanzania Stars\nWanamuziki wengine waliopitia hapo ni Mhina Panduka 'Toto Tundu' na Emma Mkelo 'Lady Champion'. Kibao cha kwanza walichoibuka ni ‘Penzi la Ulaghai’ kilichoimbwa na Eddy Sheggy katika sauti ya kwanza na Adam Bakari katika sauti ya tatu. Gitaa la solo lilikuwa likicharazwa na Hamza Kalala, solo namba mbili alipiga Robert Mabrish, Noordin Athumani alipiga rhythm, gitaa la bass lilipigwa na Juma Shaaban, Hassan Athumani (tumba), Kejeli Mfaume (drums) na kinanda kilikuwa kinapapaswa na Abdul Salvador. Onyesho la kwanza la bendi lilifanyika Novemba 1989 kwenye ukumbi wa Dodoma Hotel kwa ajili ya kuwaburudisha Wabunge na liliingiza jumla ya Shs. 17,000, yakiwa ni mapato makubwa zaidi kuingizwa na bendi yoyote ya dansi nchini kwa wakati huo.",
"Professor Jay\nJay na HBC walitoa albamu ya kwanza iitwayo 'Funaga Kazi' mwaka 2000. Albamu hiyo inaaminika kwamba ilileta mapinduzi makubwa sana ya muziki wa Hip Hop nchini Tanzania. Albamu hii yenye ujumbe mzito ina nyimbo kama 'Chemsha Bongo' na 'Mamsapu' ambazo zilichangia kufanya muziki wa 'Bongo Flava' kuwa wa kila rika na kupewa heshima. Kabla ya hapo muziki huo ulionekana kuwa ni muziki wa wahuni.",
"Al-Shymaa Kway-Geer\nKway-Geer ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga nchini Tanzania na aliteuliwa kuwa mbunge mnamo mwaka 2008. Hapo awali Kway-Geer alikuwa mhudumu wa ndege. Akiwa mlemavu wa ngozi (Albino), Kway-Geer ameonesha matumaini kwa watu wenye ulemavu kama yeye na kubadilisha mtazamo wa watu wengi nchini Tanzania wenye imani kuwa mtu mwenye ulemavu wa ngozi ni laana au chanzo cha kujipatia nguvu za giza. Manyanyaso kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) yameshamiri sana nchini Tanzania yakiwemo mauaji ya maalbino, kuwavamia na kukata baadhi ya viungo vyao.",
"Yataka Moyo\n\"Yataka Moyo\" ni jina la wimbo wa sita upande A kutoka katika tepu ya albamu ya \"Machozi Jasho na Damu\" ya msanii wa muziki wa hip hop kutoka nchini Tanzania, Professor Jay. Wimbo umetayarishwa na P. Funk ndani ya Bongo Records. \nKwa ujumla wake Jay anazungumzia mafanikio ya sanaa na wasanii. Katika muziki wa Tanzania imeonekana kawaida sana kwa wasanii na wanamuziki kutokuwa na kipato kinachoeleweka. Mifumo isiyosaidizi kwa tasnia nzima ya muziki wa Tanzania. \nJay anazungumzia wasanii wa zamani jinsi walivyoteseka katika kuuleta muziki wa Tanzania katika ramani inayoeleweka. Tena wengi wao wanakufa maskini huku kazi zao zikitumiwa na taasisi za serikali na watu binafsi bila faida kwa msanii. Wanaomba hakimiliki ya kazi za sanaa zao lakini majibu bado magumu. Katika wimbo anataja watu wengi maarufu tangu muziki wa rap ulivyoanza, hadi makuzi ya muziki wa dansi.",
"Upendo Nkone\nUpendo Nkone ni mwimbaji maalum wa kisasa Tanzania. Anaimba nyimbo za Mungu na sauti kubwa sana na kwaya yake wanaweza vizuri kumsaidia. Nkone alizaliwa sehemu ya Kigoma ingawa alipokuwa mtoto akahama mjini Dar es Salaam ambapo akalelewa. Sasa hizi, yeye ni mjane na ana watoto wawili. Nyimbo zake nyingi zinawaambia wajane, mayatima na wengine walio na matatizo kujipa moyo na kusonga mbele kwa furaha kwa sababu Mungu anawalinda. Ametunga nyimbo za kutosha kujaza albamu mbili na zote ni nzuri sana. Hasa nyimbo hizi ‘Usifurahi juu yangu’ na ‘Upendo wa Yesu’ zinapendwa sana na WaTanzania. Ndiyo maana yeye ni shujaa wa muziki ya injali ya sasa hizi.",
"Muziki wa Tanzania\nKwa upande wa muziki wa kizazi kipya, ukiacha wale walioanza kabla ya 2000, hapa anakuja Dully Sykes, Manzese Crew, Wandava Creek, Wehu Kumi Ngangari (W TEN N), TID, Jay Moe, Ngwair, Daz Nundaz, Madee, Mandojo na Domo Kaya, Mr. Blue, Complex, Dudu Baya, Juma Nature na FSG, A.Y., G.K., Q Chillah, MwanaFA, Lady Jay Dee na Ray C.. Jay Dee ndiye msanii wa kwanza kurekodi albamu yenye gharama kubwa mno kuliko zote tangu kuanza kwa muziki wa kizazi kipya kwa kipindi kile cha mwanzoni mwa miaka ya 2000. Ndiye aliyeanza kupiga video na Benchmark Production kwa kipindi haikuwa rahisi sana kufanya kazi na kampuni hiyo. Jay Dee na A.Y. ni wasanii wa mwanzo kabisa kuthubutu kutoka nje ya mipaka ya Tanzania katika kufanya muziki na wasanii wa nchi za nje."
] | 42
|
Kikurdi ni lugha ya wapi?
|
[
"Kikurdi\nKikurdi ni kundi la lahaja za Kiajemi zinazotumika na Wakurdi wengi (milioni 20-30 hivi) huko Mashariki ya Kati."
] |
[
"Kikuri\nKikuri (pia Kimodan au Kinabi) ni lugha ya Kiaustronesia nchini Indonesia inayozungumzwa na Wakuri kwenye kisiwa cha Papua. Mwaka wa 1982 idadi ya wasemaji wa Kikuri imehesabiwa kuwa watu 500 tu. Kwa vile Wakuri wengi wameacha lugha yao, Kikuri iko hatarini mwa kutoweka kabisa hivi karibuni. Kufuatana na uainishaji wa lugha Kikuri haijaainishwa kwa ndani zaidi.",
"Kikuria\nKikuria ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania na Kenya inayozungumzwa na Wakuria. Mwaka wa 2005 idadi ya wasemaji wa Kikuria nchini Tanzania imehesabiwa kuwa watu 430,000. Pia kuna wasemaji 260,000 nchini Kenya. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kikuria iko katika kundi la E40.\nKitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:",
"Kirufiji\nKirufiji (au \"Kiruihi\") ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Warufiji. Mwaka wa 1987 idadi ya wasemaji wa Kirufiji imehesabiwa kuwa watu 200,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kirufiji iko katika kundi la P10.\nKitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:",
"Kiluri\nKiluri ni lugha ya Kiafrika-Kiasia nchini Nigeria inayozungumzwa na Waluri. Mwaka wa 2004 idadi ya wasemaji wa Kiluri imehesabiwa kuwa watu wawili tu. Kwa hiyo lugha ya Kiluri imekaribia kutoweka kabisa. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiluri iko katika kundi la Kichadiki.",
"Kikari\nKikari ni lugha ya Kibantu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inayozungumzwa na Wakari. Mwaka wa 1996 idadi ya wasemaji wa Kikari nchini Kongo imehesabiwa kuwa watu 1000. Pia kuna wasemaji waliosambaasambaa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati. Kikari hakijaainishwa kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie.",
"Kikareli\nKikareli ni lugha ya Kifini-Kiugori nchini Urusi na Ufini inayozungumzwa na Wakareli. Mwaka wa 2010 idadi ya wasemaji wa Kikareli nchini Urusi imehesabiwa kuwa watu 25,600. Pia kuna wasemaji 10,000 nchini Ufini (1994). Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kikareli iko katika kundi la Kifini.",
"Kimeru (Tanzania)\nKimeru (au Kirwa) ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Warwa. Isichanganywe na lugha ya Kimeru nchini Kenya. Mwaka wa 1987 idadi ya wasemaji wa Kimeru imehesabiwa kuwa watu 90,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kimeru iko katika kundi la E60.",
"Kiludi\nKiludi ni lugha ya Kiurali nchini Urusi inayozungumzwa na Waludi. Mwaka wa 2012 idadi ya wasemaji wa Kiludi imehesabiwa kuwa watu 3000. Waludi wengi wanaotumia lugha ya Kirusi, na lugha imekaribia kutoweka kabisa hivi karibuni. Hata hivyo, nchini Ufini kuna jitihada za kufufua na kuendeleza lugha ya Kiludi.",
"Kikisi (Tanzania)\nKikisi ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wakisi. Isichanganywe na Kikisi-Kaskazini nchini Guinea wala na Kikisi-Kusini nchini Liberia; tena ni tofauti na Kikisii nchini Kenya. Mwaka wa 2001 idadi ya wasemaji ya Kikisi imehesabiwa kuwa watu 10,200. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie, lugha ya Kikisi iko katika kundi la G60.\nKitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:",
"Kiduri\nKiduri (pia Kimasenrempulu) ni lugha ya Kiaustronesia nchini Indonesia inayozungumzwa na Waduri kwenye kisiwa cha Sulawesi. Mwaka wa 2000 idadi ya wasemaji wa Kiduri imehesabiwa kuwa watu 127,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiduri iko katika kundi la Kisulawesi-Kusini."
] | 20
|
Bahari kuu duniani ni gani?
|
[
"Bahari kuu\nBahari Kuu (ing. \"w:ocean\") ni jina linalotumika kutaja jumla ya maeneo makubwa ya maji ya chumvi duniani yanayopakana na kufuatana kama gimba moja. Kwa maana hii bahari kuu inafunika zaidi ya theluthi mbili za uso wa dunia.",
"Bahari kuu\nBahari Kuu imegawiwa na ardhi ya mabara kwenye nusutufe ya kaskazini ya dunia lakini sehemu zake zinaungana kwenye nusutufe ya kusini. \nEneo hili kubwa huhesabiwa mara nyingi kama bahari kuu tatu yaani:",
"Pasifiki\nPasifiki ni bahari kubwa kuliko zote duniani.",
"Pasifiki\nPasifiki iko kati ya Bara la Amerika upande wa mashariki na Bara la Asia / Australia upande wa magharibi. \nEneo lake ni kilometa za mraba milioni 179.7 ambayo si bahari kubwa tu bali pia ni eneo kubwa kuliko nchi kavu yote duniani: ni karibu nusu ya uso wa dunia."
] |
[
"Bahari ya Kaspi\nBahari ya Kaspi (pia Bahari ya Qazwin- Kiajemi دريا خزر \"\"darya khazar\"\"; Kirusi Каспийское море \"\"kaspiiskoye more\"\") ni ziwa kubwa kabisa duniani lenye eno la 371,000 km² na mjao wa 78,200 km³. Liko kati ya Azerbaijan, Urusi, Kazakhstan, Turkmenistan na Uajemi.",
"Bahari kuu\nBahari kuu hushika asilimia 97% ya maji yote duniani. Hadi sasa ni asilimia 5 pekee zilizofanyiwa utafiti kamili. Kiasi cha maji yote kwenye bahari kuu ni takriban kilomita za mjazo bilioni 1.3.",
"Ganimedi (Mshtarii)\nMasi ya Ganimedi ni takriban nusu mwamba na nusu maji. Kwenye kitovu chake kuna kiini kidogo cha metali hasa chuma. Uso wake unafunikwa kote na barafu yenye unene wa mamia ya kilomita. Chini ya uso wa barafu iko bahari ya maji katika hali ya kiowevu. Kuna makadirio ya kwamba kiasi cha maji kwenye ganimedi inazidi jumla ya maji Duniani.",
"Kitu Gani\nKitu Gani ni nyimbo ya Dknob akimshirikisha Q Jay. Inatoka katika albamu ya \"Bomoa Mipango\". Nyimbo ilirekodiwa katika studio ya Mwamba Production ya Dar es Salaam, Tanzania. Nyimbo hii imekuwa kama utambulisho wa albamu hiyo ya Bomoa Mipango, ingawaje si wengi waliotegemea albamu itakwenda kwa jina hilo. Albamu imetolewa mnamo tarehe 1 Julai ya mwaka wa 2008.",
"Masai Mara\nHifadhi Mbuga ya Wanyamapori ya Kitaifa ya Masai Mara ina upana wa kilomita 1530 kieneo upande wa Kusini Magharibi mwa Kenya. Ndiyo sehemu ya Serengeti iliyo upande wa Kaskazini zaidi yenye upana wa jumla ya kilomita 25,000 kilomita kieneo. Upande wa Kusini imepakana na muga ya wanyama ya Serengeti, na upande wa magharibi na mharara wa Siria na upande wa Kaskazini Mashariki na Magharibi imepakana na maeneo ya ufugaji. Kiwango cha mvua katika mazingira haya huongezeka kuanzia kusini-mashariki-hadi magharibi, japo hubadilika kiwakati kutoka eneo moja hadi lingine na ni ya misimu miwili. Mito ya Sand, Talek na Mara ndiyo mito mikubwa ambayo hutoa maji kwenye hifadhi ya mbuga hii. Vichaka na miti iliyomea kwenye kingo za mito hufunika miteremko na vilele vya milima\nKimsingi mandhari ya hifadhi hii ni nyasi iliyowazi na mito. Eneo la Kusini Magharibi kuna vichka vya aina mbalimbli ya miti ya aina ya mwangate. Upande wa mpaka wa magharibi kuna harara(genge) la Esoit Oloololo la Bonde la Ufa, na wanyamapori wanapatikana eneo hili kwa wingi kwa sababu chemichemi ya maji hupatikana kwa urahisi na hakuna usumbufu wa watalii. Mwisho wa mpaka wa Mashariki ni kilomita 224 kutoka Nairobi, kwa hivyo, ni upande wa mashariki ndio hutembelewa na watalii sana.",
"Bahari kuu\nKiasi cha maji baharini kinajulikana kuwa kilicheza na kubadilika katika historia ya dunia. Wakati wa vipindi vya baridi duniani, kama vile enzi ya barafu, sehemu kubwa ya maji yalipatikana kwa umbo la barafu na maji kiowevu yalikuwa kidogo. . Kuongezeka kwa halijoto duniani kunasababisha kupanda kwa uwiano wa bahari kote duniani. Nchi mbalimbali hasa kwenye pwani au nchi za visiwa zitapungua kieneo.",
"Mirihi\nMirihi ni sayari iliyoaminika kuwa na uhai hata aina ya wanadamu. Tofauti na sayari nyingine jirani na dunia yetu, ambayo ni Zuhura (au Ng'andu), uso wa Mirihi unaonekana kwa darubini. Katika karne ya 19 BK wanaastronomia, hasa Mwitalia Giovanni Schiaparelli, waliona alama kama mistari kwenye uso wa Mirihi. Schiaparelli aliita mistari hii kwa neno la Kiitalia \"canali\" yaani mifereji. Jina hili lilisababisha watu wengi kujiuliza: mifereji imepatikana namna gani? Halafu katika eneo la mistari hii mabadiliko ya rangi ilionekana. Haya yote yamesababisha dhana na makadirio ya kuwa mifereji imechimbwa kwa kusudi la kupeleka maji maeneo makavu yanayomwagiliwa na kuonyesha rangi ya mazao kimajira. Kumbe lazima kuwe na wachimbaji, kwa hiyo wako aina ya watu wenye utamaduni. Watu hao waliozaliwa katika fikra za wanaastronomia na waandishi wa vitabu walijulikana kote duniani; baadaye imani ilianza ya kuwa wanatutembelea duniani.",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nKuongezeka kwa asidi baharini ni chanzo cha ukolezi wa kiwango cha CO katika anga, na si matokeo ya moja kwa moja ya ongezeko la joto Duniani. Bahari huchukua ndani kiasi kikubwa cha CO kinachotolewa na viumbe hai, kama gesi mmunyufu au katika mifupa ya wanyama wadogo wa majini ambao huanguka chini na kuwa chokaa au simiti. Bahari kwa sasa huchukua karibu tani moja ya CO kwa kila mtu kila mwaka. Inatabiriwa kuwa bahari imechukuwa ndani karibu nusu ya CO inayozalishwa na shughuli za kibinadamu tangu mwaka wa 1800 (petagramu 118 ± 19 za kaboni tangu mwaka wa 1800 hadi mwaka wa 1994)."
] | 6
|
Je,mji wa Gold Coast inapatikana nchi gani?
|
[
"Gold Coast\nTangu 1919 gavana aliwajibika pia kwa sehemu ya Togo ya Kiingereza (maeneo ya Togo ya Kijerumani ya awali zilizokabidhiwa kwa Uingereza) iliyotawaliwa kama \"Togo ng'ambo ya mto Volta\". Wakati wa mwisho wa ukoloni wakazi wengi wa sehemu hiyo walipiga kura ya kujiunga na Gold Coast na sasa ni sehemu kamili ya Ghana.",
"Guinea (kanda)\nLugha za Ulaya zilikuwa na majina ya kihistoria kwa ajili ya sehemu mbalimbali za pwani la Guinea ya Juu: Pwani la Pilipili (ing. \"Pepper Coast\"), Pwani la Meno ya Ndovu (ing. \"Ivory Coast\"), Pwani la Dhahabu (ing. Gold Coast) na Pwani la Watumwa (ing. \"Slave Coast\"). Majina haya yametokana na biashara kuu katika sehemu zile. Jina la \"Pwani la Meno ya Ndovu\" linaendelea kutumika katika nchi ya Cote d'Ivoire (Ivory Coast). Ghana lilitwa \"Gold Coast\" (Pwani la Dhahabu) hadi uhuru.",
"Gold Coast\nGold Coast (kwa Kiswahili: Pwani ya Dhahabu) ilikuwa jina la koloni la Uingereza katika Afrika ya Magharibi kwenye mwambao wa Ghuba ya Guinea ambalo limekuwa nchi ya Ghana tangu uhuru wake (1957).",
"Hastings Banda\nBaada ya miaka kadhaa huko Gold Coast (Ghana) aliombwa na wanasiasa Waafrika arudi Nyasaland akafika mwaka 1958. Kwenye mkutano wa chama cha Nyasaland African Congress (NAC) alichaguliwa mara moja kuwa kiongozi. Alikuta nchi yake Nyasaland kuwa sehemu ya Shirikisho la Afrika ya Kati ambako walowezi wa Rhodesia ya Kusini walikuwa na athira kubwa na kuendeleza ubaguzi wa rangi. Banda alipinga kuwepo kwa shirikisho hili.",
"Ghana\nBaada ya Waholanzi kuondoka mwaka wa 1874, Uingereza iliiweka Gold Coast chini ya himaya yake. Kufuatia ushindi wa Uingereza mwaka wa 1896, hadi unyakuzi wa uhuru mnamo Machi 1957, eneo la Ghana ya sasa ghairi ya sehemu ya Volta Region (British Togoland), lilikuwa likijulikana kama Gold Coast."
] |
[
"Dubai Gold Souk\nDubai Gold Souk (Kiarabu: دبي سوق الذهب au Gold Souk) ni soko la jadi lililopo mjini Dubai. Soko hili lipo mjini mashariki mwa Dubai katika sehemu za biashara wilayani Deira. Kuna zaidi ya wauzaji 300 wanaofanya biashara. Kuna maduka ya rejareja katika soko hili yanayojulikana kama Damas, ARY jewellery, Prima Gold na Joy Allukas jewellery. Vilevile kuna maduka madogo madogo yanayojihusisha na biashara ya dhahabu pekee yake. Dubai Gold Souk iko katika maeneo ya Al Dhagaya. Kwa kutumia makadirio, takriban tani 10 za dhahabu hupatikana wakati wowote katika \"Souk\" . Mipaka yake ya kaskazini ni Dubai Fish na Vegetable Market na Deira Corniche.\nBiashara katika \"Soko\" hili la dhahabu iliimarishwa wakati wa miaka ya 1940 kutokana na mfumo wa Dubai wa kuruhusu biashara huria iliyovutia wanabiashara kutoka India na Iran kuanzisha maduka katika \"Soko\" hilo. Hata kama bei ya dhahabu ilizorota kote duniani katika soko la kimataifa, thamani ya biashara ya dhahabu na almasi kwa jumla njini Dubai, isiyo ya moja kwa moja na biashara ya mafuta, iliongezeka kutoka 18% mwaka 2003, hadi 24% mwaka 2004. Mwaka 2003, thamani ya biashara ya dhahabu mjini Dubai ilikadiriwa kuwa Dirhamu Bilioni 21 (dola bilioni 5.8), wakati biashara ya almasi ilikadiriwa kuwa Dirhamu Bilioni 25 (Dola bilioni 7) mwaka 2005. India ni mnunuzi mkubwa kabisa wa dhahabu, ikikadiria wastani wa 23% (2005) kwaa jumla ya dhahabu mjini Dubai katika biashara ya mwaka 2005. Uswisi ulikuwa msambazaji mkubwa wa dhahabu iliyomo Dubai. Vilevile, Bara Hindi ilikuwa na wastani wa 68% ya almasi yote inayohusiana na biashara mjini Dubai; Ubelgiji ikikadiriwa kuwa takriban ya 13% katika biashara ya almasi mjini Dubai (2005).",
"Ghana\nGhana ni nchi ambayo inapatikana katika Ghuba ya Guinea, nyusi chache kaskazini mwa Ikweta, jambo ambalo linaipa nchi hii hali ya joto. Nchi hii inapatikana katika eneo la kilomita mraba 238,500 (maili mraba 92,085). Eneo hili limezungukwa na Togo kwa upande wa mashariki, Cote d’Ivoire upande wa magharibi, Burkina Faso upande wa kaskazini na Ghuba ya Guinea (Bahari ya Atlantiki) upande wa kusini. Laini ya Greenwich Meridian hupita ndani ya Ghana, katika jiji la viwanda la Tema. Kijiografia Ghana inapatikana karibu zaidi ya sehemu ya “katikati” mwa ulimwengu kuliko nchi yoyote ile ingawa sehemu halisi ya katikati, (0°, 0°) inapatikana katika Bahari ya Atlantiki kwa makadirio kilomita 614 (maili 382) kusini mwa Accra, Ghana, katika Ghuba ya Guinea.",
"Ghana\nWafanyabiashara wengine kutoka Ulaya walijiunga nao kufikia miaka ya kati ya karne ya 17, hasa Waingereza, Wadenmarki na Waswidi. Wafanyabiashara Waingereza, waliovutiwa na rasilimali katika eneo hilo, waliliita \"Gold Coast,\" (Pwani ya Dhahabu), huku nao wafanyabiashara Wafaransa, wakivutiwa na mapambo waliyokuwa wakivaa watu wa pwani, wakiliita eneo la sehemu ya magharibi “Côte d'Ivoire\", au Ivory Coast (pwani ya pembe za ndovu).",
"Gold Coast\nMnamo 1902 maeneo upande wa kaskazini wa Ashanti yaliongezwa kufuatana na mapatano na Ujerumani na Ufaransa. Kwa hiyo sehemu tatu za Gold Coast yenyewe, Ashanti na maeneo ya kaskazini yalikuwa koloni moja chini ya gavana wa Accra.",
"Gorée\nGorée (kifaransa: \"Île de Gorée\") ni kisiwa cha Atlantiki mbele ya pwani la Senegal na sehemu ya manisipaa ya Dakar. Ilijulikana kama kituo cha biashara ya watumwa. Hadi kukomeshwa kwa biashara hiyo mwaka 1848 watumwa walipelekwa kisiwani kutoka bara, kufungwa katika majela, kuuzwa kwenye minada na kubebwa Amerika kwa jahazi.",
"Ghana\nBendera iliyokuwa na rangi nyekundu, dhahabu, kijani kibichi na nyota nyeusi ilikuwa bendera mpya mnamo 1957. Bendera hiyo iliundwa na Theodosia Salome Okoh, na rangi nyekundu inawakilisha damu iliyomwagwa ili kupata uhuru, rangi ya dhahabu inawakilisha ukwasi wa madini wa Ghana, ile ya kijani kibichi inaashiria utajiri wa kilimo na ile nyeusi ni ishara ya Uhuru wa Waafrika."
] | 43
|
Mji mkuu wa Hawaii unaitwaje?
|
[
"Honolulu, Hawaii\nHonolulu ndiyo mji mkuu katika jimbo la Hawaii. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2000, mji una wakazi wapatao 900,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 0 kutoka juu ya usawa wa bahari.",
"Hawaii\nMji mkuu ni Honolulu kwenye kisiwa cha Oahu."
] |
[
"Papa Mbingusi\nKatika utamaduni wa asili wa Hawaii, papa wanachukuliwa kuwa miungu ya bahari, walinzi wa wanadamu, na wasafishaji wa bahari dhidi viumbe vya ziada. Baadhi ya hawa papa wanaaminika kuwa wanafamilia ambao walikufa na kuzaliwa upya katika umbo la papa. Hata hivyo, baadhi ya Papa huchukuliwa ni wala watu, pia wanajulikana kama niuhi. Papa hawa ni pamoja na papa mweupe mkubwa, papa ngusi na papa-fahali. Papa mbingusi, anayejulikana pia kama \"mano kihikihi\", hachukuliwi kama mla watu au \"niuhi\"; anachukuliwa kuwa moja ya papa mwenye kuheshimiwa zaidi baharini, ni aumakua. Familia nyingi za Hawaii huamini kuwa wanaye aumakua anayewaangalia na kuwalinda dhidi ya niuhi. Papa mbingusi anafikirika kuwa ni mnyama wa uzazi kwa baadhi ya watoto. Watoto wa Hawaii ambao huzaliwa na papa mbingusi kama ishara ya mnyama wanaaminika kuwa askari mashujaa na wamemaanishwa kusafiri baharini. Ni nadra sana kwa papa mbingusi kupita maji ya \"Maui\", lakini wenyeji wengi wa Maui huamini kwamba papa mbingusi akipita kuogelea ni ishara kwamba miungu wanazichunga familia zao, na bahari ni safi na tulifu.",
"Mji mkuu\nKwa nia hiyohiyo Tanzania iliamua kuhamisha mji mkuu kutoka Daressalaam uliyoko pwani la Bahari Hindi kwenda Dodoma iliyoko katikati ya Tanzania. Uhamisho huu umepangwa tangu 1967 na kutangazwa rasmi mwaka 1997 lakini haujatekelezwa bado. Ni ofisi chache za serikali zimehamia hapo. Watanzania wanaochoka na kuchelewe huku waangalie mfano wa Brazil: Katiba ya Brazil ya mwaka 1891 ilishataja mahali pa mji mkuu mpya badala ya Rio de Janeiro lakini mipango haikuanza hadi 1926 halafu ujenzi ulianza 1956!Uturuki iliamua 1923 kuhamisha mji mkuu kutoka Istanbul kwenda Ankara. Istanbul iliwahi kuwa kwa karne nyingi mji wa Masultani tena mji wa kimataifa; mapinduzi ya 1923 yalimaliza utawala wa sultani na kutangaza Uturuki kuwa jamhuri. Pia Istanbul imekuwa kandokando ya eneo la Uturuki baada ya vita kuu ya kwanza kwa sababu sehemu za magharibi zilikuwa zimepotea na kuchukuliwa na Wagiriki na Wabulgaria. Hivyo Ankara iliteuliwa iliyoko katikati ya Uturuki mpya baada ya vita.",
"Milima Makaleha\nMilima Makaleha (inayojulikana kama [mɐkəlɛhə] au [mɐtəlɛhə] katika Kihawaii) ni safu ya milima ambayo ipo katika kata ya Kauai upande wa mashariki wa funguvisiwa la Hawaii kilichopo Kauai.",
"Arusha (mji)\nMji wa Arusha una kiwanja cha kimataifa cha ndege cha Kilimanjaro kinachopatikana kilomita 60 mashariki ukielekea Moshi kwa ajili ya wasafiri wa kimataifa. Kuna ndege za kimataifa na za ndani. Uwanja wa ndege wa Arusha ni uwanja mdogo magharibi mwa mji, kwa sasa wanaendelea na upanuzi wa uwanja huu. Uwanja huu una abiria 87,000 kila mwaka licha ya udogo wake.",
"Nuku Hiva\nNuku Hiva ni kisiwa cha Polinesia ya Kifaransa. Kiko upande wa magharibi wa kisiwa cha Ua Huka. Eneo la kisiwa ni 339 km². Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Taiohae. Mwaka wa 2007, idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa 2660. Watu wakaao kisiwani kwa Nuku Hiva huongea Kimarkesa ya Kaskazini na Kitahiti.",
"Mbeya (mji)\nMji ulianzishwa katika sehemu zinazoitwa bado Uhindini, Uzunguni na Majengo. Mji ulipangwa kufuatana na kawaida ya miji wa kikoloni ya Afrika ya Mashariki kuwa na sehemu tatu:Mahali pa makanisa ya kale panaonyesha ugawaji huu wa kihistoria:",
"Kenya\nWadhifa huo mpya wa waziri mkuu utakuwa na nguvu na mamlaka kuratibu na kusimamia shughuli za serikali. Vilevile itaongozwa na mbunge aliyechaguliwa ambaye pia atakuwa kiongozi wa chama au muungano wa vyama wenye idadi kubwa ya wabunge bungeni. Ulimwengu ulimshuhudia Annan na kamati yake iliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na mwenye kiti wa muungano wa nchi za Afrika Jakaya Kikwete, walipowaleta pamoja wapinzani hawa sugu kwenye sherehe za kutia sahihi mkataba huu. Sherehe hizi zilionyeshwa moja kwa moja kwenya televisheni ya kitaifa kutoka kiingilio cha Jumba la Harambee mjini Nairobi. Wawakilishi wa PNU na ODM walianza majadiliano ya kina kuhusu ugavi wa mamlaka tarehe 29 Februari 2008. Wabunge wa Kenya, kwa pamoja, waliidhinisha mkataba wa ugawaji mamlaka tarehe 18 mwezi wa Machi 2008 ili kuiokoa Kenya iliyoaminika kama mojawapo ya nchi thabiti na iliyoendelea barani Afrika. Mkataba huu uliunganisha PNU iliyoongozwa na Kibaki na ODM ya Odinga kisha kupelekea kuundwa kwa serikali ya muungano, vyama vyote viwili vikiwa na mamlaka sawa.",
"Kauehi\nKauehi ni kisiwa cha Polinesia ya Kifaransa ndani ya funguvisiwa ya Tuamotu. Kiko upande wa kaskazini-mashariki wa kisiwa cha Fakarava. Eneo la kisiwa ni 15 km². Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Tearavero. Mwaka wa 2012, idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa 257. Watu wakaao kisiwani kwa Kauehi huongea Kituamotu na Kitahiti."
] | 36
|
Carleton Gajdusek alisoma udaktari chuo gani kikuu?
|
[
"Carleton Gajdusek\nBaba yake Gajdusek, Karol Gajdusek, alitoka Smrdáky, Ufalme wa Hungaria ambayo sasa inapatikana Slovakia. Karol alikuwa Mslovakia na alifanya kazi ya uchinjaji. Wazazi wa mama yake, waliokuwa Wahungaria na Wakalvini, walihama kutoka Debrecen, Hungaria. Gajdusek alizaliwa Yonkers, New York, na akahitimu kutoka Chuo Kikuu cha Rochester mwaka wa 1943 aliposoma fizikia, biolojia, kemia na hisabati."
] |
[
"Catherine Ruge\nAlisoma Shule ya Sekondari Msalato mkoani Dodoma kuanzia mwaka 2001 hadi 2003. Baadaye alisoma Jangwani kuanzia Juni 2001 hadi Mei 2003 na kuhitimu elimu ya juu ya sekondari. Alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 2004 hadi 2007 akisomea Shahada ya Biashara na Uhasibu. Mwaka 2011 – 2015 alisoma Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Biashara katika chuo cha ESAMI (Eastern and Southern Africa Management Institute). Kwa sasa anachukua masomo ya udaktari (PHD) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye masuala ya jinsia katika fani ya uhasibu.",
"Carleton Gajdusek\nCarleton Gajdusek (amezaliwa 9 Septemba 1923) alikuwa daktari kutoka nchi ya Marekani. Baadhi ya utafiti mwingine hasa alichunguza maradhi za neva. Mwaka wa 1976, pamoja na Baruch Blumberg alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.",
"Carleton Gajdusek\nMwaka wa 1966, Carleton Gajdusek alipatikana na hatia ya udhahilishaji wa watoto na akafungwa miezi 12 gerezani kabla ya kuhama kuenda Ulaya, alipokufa miaka kumi baadaye.",
"Carleton Gajdusek\nMaandishi yake yamehifadhiwa katika Maktaba ya Udaktari ya Taifa ya Marekani, mji wa Bethseda, Maryland.",
"Jost Gippert\nMwaka wa 1997 aliteuwa profesa wa heshima katika chuo kikuu \"Sulkhan Saba Orbeliani\", mji wa Tbilisi (Georgia), na 2009 aliteuwa udaktari wa heshima katika chuo kikuu \"Ivane Javakhishvili\", mahali sawasawa. Na mwaka wa 2013 aliteuwa udaktari wa heshima katika chuo kikuu \"Shota Rustaveli\", mji wa Batumi (Georgia). Kazi zake muhimu kama profesa kwa isimu ya mlingo katika Frankfurt, licha ya uchunguzi wa lugha za Kihindi-Kiulaya na mgawanyiko jenerali wa lugha, ni uchunguzi wa lugha za Caucasus. Miradi mingine ya kimataifa imefanyiwa chini ya usimamizi wake.",
"Baruch Blumberg\nBaruch Samuel Blumberg (amezaliwa 28 Julai 1925) alikuwa daktari kutoka nchi ya Marekani. Hasa alichunguza damu ya watu. Mwaka wa 1976, pamoja na Carleton Gajdusek alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.",
"Jost Gippert\nMwaka wa 1972 alihitimu masomo ya sekondari katika \"Leibniz-Gymnasium\", katika mji wa Essen-Altenessen. Tangu 1972 mpaka 1977 alijifunza isimu wa mlingo, usayansi wa India, usayansi wa Japan na usayansi wa China katika chuo kikuu Marburg na chuo kikuu huru Berlin. Baada ya masomo aliupata udaktari wa Falsafa (Ph.D.) kwa kazi yake kuhusu \"Syntax of infinitival formations in the Indo-European languagues\". Tangu 1977 mpaka 1990 alifanya kazi nyingine kama mwanamaarifa na alifanya madarasa katika Berlin, Vienna na Salzburg. Mwaka wa 1991, alipofanya kazi kama mwanamaarifa kwa isimu ya mashariki ya kompyuta, yeye alifanya katika chuo kikuu mji wa Bamberg kwa kazi yake kuhusu \"Iranian loanwords in Armenian and Georgian\". Jost Gippert afundisha isimu ya mlingo katika chuo kikuu \"Johann-Wolfgang-Goethe\", Frankfurt, tangu 1994. Tangu 1996 yeye ni mwanachama mgeni wa „Gelati Science Academy“ (Georgia). Tangu 2002 yeye ni mwanachama wa \"Tufankommission\"; na tangu 2007 ni mwanachama wa Katikati \"Lugha\" ya Chuo cha Sayansi Berlin-Brandenburg (Berlin-Brandenburg Science Academy).",
"Constantine John Kanyasu\nAlijiunga na JKT Bulombola na baadaye alisoma uvuvi kabla ya kujiunga na chuo kikuu huria kwa digrii ya kwanza na baadaye SAUT Mwanza kwa digrii ya pili.",
"Al-Shymaa Kway-Geer\nKway-Geer ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga nchini Tanzania na aliteuliwa kuwa mbunge mnamo mwaka 2008. Hapo awali Kway-Geer alikuwa mhudumu wa ndege. Akiwa mlemavu wa ngozi (Albino), Kway-Geer ameonesha matumaini kwa watu wenye ulemavu kama yeye na kubadilisha mtazamo wa watu wengi nchini Tanzania wenye imani kuwa mtu mwenye ulemavu wa ngozi ni laana au chanzo cha kujipatia nguvu za giza. Manyanyaso kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) yameshamiri sana nchini Tanzania yakiwemo mauaji ya maalbino, kuwavamia na kukata baadhi ya viungo vyao."
] | 54
|
Mji mkuu wa Norway unaitwaje?
|
[
"Bergen\nBergen ni mji wa pili kwa ukubwa nchini Norwei. Mji una wakazi takriban 262,500 kulingana na makisio ya 31 Julai 2011. Bergen ni kitovu cha ngazi ya utawala ya jimbo la Hordaland. Maeneo ya Mji Mkuu wa Bergen kama yalivyoelezwa na Statistics Norway, una wakazi 386,400 ifikapo 31 Julai 2011.",
"Norwei\nMji mkuu ni Oslo."
] |
[
"Magharibi mwa Norwei\nMagharibi mwa Norwei () ni kanda iliyopo katika pwani ya bahari ya Atlantiki huko mjini kusini mwa nchi ya Norwei. Kanda ina-jumlisha baadhi ya majimbo kama vile Rogaland, Hordaland, Sogn og Fjordane, na Møre og Romsdal na kanda ina wakazi wapatao milioni 1.3. Mji mkubwa kabisa katika kanda hii ni Bergen, wa pili kwa ukubwa ni Stavanger. Agder, Vest-Telemark, Hallingdal, Valdres na sehemu za kaskazini mwa Gudbrandsdal zilikuwa katika jimbo hili wakati wa kupanga Magharibi mwa Norwei.",
"Norrköping\nNorrköping ni mji kubwa nchini Uswidi. Ni mji mkubwa wa kumi katika nchi wa Uswidi. Kuna wakazi 83,561 (mwaka 2005). Iko kando ya Mto Motala. Kuna bendi simfoni, uwanja wa ndege na tawi la Chuo Kikuu cha Linköping",
"Hedmark\nJimboni humo miji mashuhuri iliyojengwa ni pamoja na Hamar, Kongsvinger, Elverum na Tynset. Hedmark ni moja kati maeneo ambayo hayakujengwa sana nchini Norwei, kama jinsi ilivyo nusu ya wakazi wake wanaishi katika maeneo ya vijijini. Uwingi wa watu hutazamwa sana kule katika maeneo ya matajiri ambapo ni Mjøsa na pande zingine za kusini-mashariki. Misitu mikubwa ya jimboni hapa inasambaza mbao vya kutosha nchini Norwei; vigogo vilikuwa vikisafirishwa kupitia Glomma kwa njia ya bahari lakini siku hizi vinasafirishwa kwa njia ya lori au treni.",
"Wellington\nWellington ni mji mkuu wa Nyuzilandi mwenye wakazi 350,000 (2005). Iko upande wa kusini wa kisiwa cha kaskazini ikitazama milima ya kisiwa cha kusini. Imekuwa mji mkuu tangu 1865 ilipochukua nafasi ya Auckland. Mji wa Wellington umekuwa maarufu sana kwakuwa filamu ya The Lord of the Rings ilitengenezwa katika mji huo.",
"Mji mkuu\nNigeria iliamua mwaka 1976 kuhamisha mji mkuu wa kitaifa kutoka Lagos kwenda mahali pa katikati ya nchi. \"Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho\" limeteuliwa. Mji mpya wa Abuja ndani ya eneo hili ukawa mji mkuu wa Nigeria mwaka 1991.",
"Norwei\nMji mkuu wake una wakazi wanaozidi 530,000. Miji mingine mikubwa ni pamoja na Bergen wenye wakazi 230,000 na Trondheim wenye wakazi 150,000; yote miwili imewahi kuwa miji mikuu ya Unowe katika miaka ya mwanzoni.",
"Buskerud\nBuskerud ni moja kati ya Majimbo ya Norwei. Jimbo limepakana na Akershus, Oslo, Oppland, Sogn og Fjordane, Hordaland, Telemark, na Vestfold. Ngazi ya utawala ya jimboni hapa ipo mjini Drammen.\nBuskerud inaanzia kutoka Hurum katika Oslofjord hadi katika milima ya Halling na Hardanger. Kikawaida jimbo hugawanyika katika wilaya za zamani. Ambazo ni Eiker, Ringerike, Numedal na Hallingdal. Hønefoss ni wilaya kuu ya Ringerike.Upande wake wa magharibi ni milima na mabonde Uwanda wa misitu na ya juu, malisho ya nyasi; sehemu yake ya mashariki ina bonde tambarare na maziwa mengi na mito. Tyrifjorden na Krøderen ni miongoni mwa maziwa makubwa. Numedalslågen, ziwa la tatu ambalo ni refu sana nhini Norwei, linanza mjini Hordaland, linapitia Buskerud hadi Vestfold ambapo inakutana na bahari, wakati mto Begna unamwagikia katika ziwa Sperillen.",
"Niamey\nNiamey ni mji mkuu wa Niger. Iko mwambaoni wa mto Niger. Ikiwa na wakazi 674,950 (sensa ya 2002) Niamey ni mji mkubwa wa Niger na kitovu cha kiutawala, kiuchumi na kiutamaduni.",
"Rize\nRize ni jina la kutaja mji mkuu wa Mkoa wa Rize huko nchini Uturuki. Mji upo mjini kaskazini-mashariki mwa pwani ya Bahari Nyeusi. Mji una wakazi takriban 78,144 wanaoishi mjini hapa. Mji upo 6 kutoka juu ya usawa wa bahari."
] | 19
|
Rais wa kwanza wa Malawi ni nani?
|
[
"Malawi\nMalawi ilikuwa na siasa ya chama kimoja chini ya rais wa kwanza Hastings Kamuzu Banda tangu kupata uhuru mwaka 1964 na masahihisho ya katiba 1966.",
"Malawi Congress Party\nBadala yake viongozi wa awali wa NAC wasiokuwa gerezani waliunda Malawi Congress Party (MCP) iliyomtambua Hastings Banda kuwa kiongozi wake ilhali amefungwa jela."
] |
[
"Siasa ya Malawi\nChini ya Katiba ya 1995, rais ambaye pia ni Kiongozi wa Nchi na kiongozi wa Serikali anachaguliwa na raia baada ya kipindi cha miaka mitano. Malawi ina Makamu wa Rais ambaye huchaguliwa na rais mwenyewe. Rais pia ana nafasi ya kumchagua makamu wa rais wa pili, ambaye lazima awe katika chama tofauti. Wanachama wa Baraza la Mawaziri wanaweza kuteuliwa miongoni mwa, au nje ya Bunge. Baraza hili huchaguliwa na rais.",
"Uchaguzi Mkuu wa Malawi, 2004\nKufikia 22 Mei, hakuna matokeo yalikuwa yametangazwa, jambo lililoonekana kutishia amani. Mnamo 25 Mei, Tume ya Uchaguzi ya Malawi hatimaye ilitangaza matokeo. Bingu wa Mutharika, mgombezi wa urais kwa chama cha United Democratic Front, alitangazwa kuchaguliwa. Mutharika alikuwa akiungwamkono na rais anayeondoka Bakili Muluzi, ambaye alisaafu baada ya kuhudumu kwa vipindi viwili. Malawi haina Kura za maoni za kutegemewa lakini utafiti uliofanywa na vyombo vyya habari vya Malawi kabla ya uchaguzi ulikuwa umemweka Gwanda Chakuamba, mgombea wa mrengo wa vyama saba kuwa aliyepigiwa upato kuongoza.\nBunge la Malawi lina wabunge 192. Kulingana na BBC, Chama cha Malawi Congress kilishinda viti ‘’’60’’’, United Democratic Front kikashinda 49, Muungano wa Mgwirizano ukazoa viti 28 na wagombea wa kibinafsi wakanyakua viti 38. Katika Uchaguzi Mkuu wa Malawi wa 1999, United Democratic Front ilikuwa imeshinda viti 93, Malawi Congress Party kikashinda viti 66, huku Alliance for Democracykikishinda viti 29.",
"Malawi\nKatika Unyasa daktari Hastings Kamuzu Banda alijitokeza kuwa mwanasiasa aliyependelewa na wananchi wengi, akawa waziri mkuu wakati wa Unyasa kupata madaraka ya kujitawala katika mambo ya ndani na baadaye rais wa kwanza wa taifa.",
"Rais wa Afrika ya Kusini\nRais anachaguliwa na wabunge wa kitengo cha chini \"(National Assembly)\" cha Bunge la Afrika Kusini. Kwa kawaida huwa kiongozi wa chama kikubwa zaidi bungeni, ambacho kimekuwa African National Congress tangu uchaguzi wa kwanza baada ya kupinduliwa kwa apartheid (ubaguzi wa rangi) uliyofanyika tarehe 27 Aprili 1994. Rais wa kwanza kuchaguliwa chini ya katiba mpya alikuwa Nelson Mandela, ambaye alifuatwa na Thabo Mbeki mwaka wa 1999, kufuatiwa na Kgalema Motlanthe mnamo Septemba 2008 na kisha Jacob Zuma mnamo Mei 2009. Katika § 5, sehemu ya 88, katiba inaruhusu wakati wa Rais ofisini kuwa muhula miwili. Marais huchaguliwa kila baada ya uchaguzi wa wabunge, na uchaguzi huu huwapa marais muda wa miaka mitano, pamoja na nafasi ya kurudishwa mara moja.",
"Siasa ya Malawi\nBakili Muluzi alikuwa rais wa Malawi kuanzia 21 Mei 2004, huku akiwa ameshinda tena baada ya kushinda uchaguzi wa 2000 na asilimia 51.4 ya kura, akimshinda mpinzani wake wa karibu zaidi Gwandaguluwe Chakuamba ambaye alikuwa na asilimia 44.3 kutoka chama cha MCP-AFORD. Mnamo 2004, Bingu wa Mutharika alimshinda tena Chakwamba kwa tofauti ya alama kumi.",
"Malawi\nKutokana na katiba ya 1995 rais wa taifa anayechaguliwa na wananchi ndiye mkuu wa dola pia mkuu wa serikali. Makamu wa rais anachaguliwa pamoja naye lakini rais ana haki ya kumteua makamu wa pili asiyetoka katika chama chake.",
"Historia ya Malawi\nKatika Unyasa daktari Hastings Kamuzu Banda alijitokeza kuwa mwanasiasa aliyependelewa na wananchi wengi, akawa waziri mkuu wakati wa Unyasa kupata madaraka ya kujitawala katika mambo ya ndani na baadaye rais wa kwanza wa taifa.",
"Simeon Nyachae\nNyachae alistaafu kutoka kwa utumishi wa umma mnamo mwaka wa 1987 akaanza kujenga maisha yake ya kisiasa. Katika mwaka 1992 alichaguliwa mara ya kwanza kama mbunge wa Nyaribari Chache na Rais Moi akamteua kuwa Waziri wa Kilimo. Mwaka wa 1997 akawa Waziri wa Fedha. Mwaka mmoja baadaye, Rais Moi alimteua kama Waziri wa Usitawi na Nyachae akakataa na kujiuzulu kama Waziri na pia kutoka chama cha KANU, na akjiunga na Ford-People, chama kidogo cha upinzani, kilicho na ushawishi wa wanasiasa wa kutoka katika mkoa wa Kati.",
"Jamhuri ya Watu wa Zanzibar\nRais Amani Abeid Karume ambaye ni mwana wa rais wa kwanza na alikuwa mgombea wa CCM alichaguliwa mara ya pili na wananchi wote tarehe 30 Oktoba 2005 katika kura iliyopingwa na chama cha upinzani CUF."
] | 56
|
Je, Adolf Hitler alikuwa anatoka nchi gani?
|
[
"Benito Mussolini\nDikteta Mjerumani Adolf Hitler alikuwa amevutwa na siasa ya Mussolini akamwiga katika mengi. Lakini Mussolini hakumpenda Hitler, hasa itikadi yake ya kimbari. Alikuwa na wasiwasi kuhusu mipango ya Hitler dhidi ya Austria. Mwaka 1934 alituma wanajeshi mpakani mwa Austria akiogopa uvamizi wa Wajerumani katika nchi ya jirani.",
"Adolf Hitler\nChuki dhidi ya Wajerumani waliokuwa Wayahudi aliionyesha kwa sheria mbalimbali zilizokuwa kali zaidi na zaidi. Idadi ya Wayahudi katika Ujerumani ilikuwa ndogo, takriban nusu milioni kati ya wakazi milioni 62. Kila Mjerumani akitaka kuajiriwa na serikali au kupata nafasi ya masomo alitakiwa kuorodhesha wazazi na mababu hadi kizazi cha pili. Kwa njia hiyo Hitler alipanga Wajerumani wote katika vikundi vya \"Waaria\" (ambao hawana Wayahudi katika familia), \"Wayahudi\" (watu wenye asili ya Kiyahudi, hata kama wameshakuwa Wakristo tangu vizazi kadhaa au hawakufuata dini), \"Wayahudi nusu\" kama mzazi mmoja alikuwa Myahudi, \"Wayahudi robo\" kama mmoja kati ya mababu na mabibi wanne alikuwa Myahudi. Wayahudi na Wayahudi nusu walifukuzwa katika ajira ya serikali na walikataliwa kufanya kazi mbalimbali.",
"Urusi\nMwaka 1939, mwanzoni mwa vita kuu ya pili ya dunia Stalin alipatana na Ujerumani wa Adolf Hitler kugawa maeneo ya Poland na nchi za Baltiki kati yao lakini mwaka 1941 Hitler alishambulia pia Umoja wa Kisovyeti.",
"Historia ya Urusi\nMwaka 1939, mwanzoni mwa vita kuu ya pili ya dunia Stalin alipatana na Ujerumani wa Adolf Hitler kugawa maeneo ya Poland na nchi za Baltiki kati yao lakini mwaka 1941 Hitler alishambulia pia Umoja wa Kisovyeti."
] |
[
"Adolf Hitler\nTangu 1910 Hitler alikuwa na mapato madogo kwa njia ya kunakili picha alizouza kupitia watu walioishi pamoja naye katika bweni. Wengine waliouza picha kwa niaba yake walikuwa Wayahudi lakini, tofauti na daktari wa mamake, hakuwapa usaidizi wowote baadaye: waliteswa kama Wayahudi wote baada ya kuvamiwa kwa Austria 1938.",
"Adolf Hitler\nTangu 1906 Hitler alijisikia kuwa msanii alipeleleza nafasi za kusoma uchoraji. Mwaka 1907 aliomba kupokewa katika chuo cha sanaa mjini Vienna, lakini alishindwa. Akarudi nyumbani baada ya kusikia mamake alikuwa mgonjwa wa kansa. Aliangalia nyumba hadi kifo cha mama kwenye Desemba 1907. Mama alitibiwa na daktari Eduard Bloch aliyekuwa Myahudi; Adolf alimshukuru sana kwa juhudi zake na baadaye alimlinda Bloch dhidi ya mateso yaliyoandaliwa kwa Wayahudi katika miaka ya 1930 baada ya Hitler kuwa mtawala wa Ujerumani na tangu 1938 wa Austria pia.",
"Adolf Hitler\nTarehe 25 Aprili 1945 Berlin yote ilizungukwa kama kisiwa na jeshi la Wasovyeti na tangu 28 Aprili waliingia katika kitovu cha Berlin. Habari zilifika Berlin ya kwamba makamu wake Hitler kama Himmler na Goering walijaribu kutafuta mapatano na Marekani au Uingereza. Hitler aliwatangaza ni wasaliti akaamuru kuwakamata lakini amri hizi hazikutekelezwa tena maana hawakuwa karibu naye.",
"Adolf Hitler\nKatika hali hii Hitler alielewa ya kwamba hakuna njia ya kushinda na wataalamu hukubaliana ya kwamba hapo aliamua kujiua. Usiku wa 27 Aprili alimwoa mpenzi wake wa miaka mingi Eva Braun. Aliendelea kutunga wosia wake ambamo alimtaja mkuu wa jeshi la maji Karl Doenitz kuchukua madaraka yake kama mkuu wa dola na wa jeshi. Kwenye 29 Aprili jioni alipokea habari ya kwamba Benito Mussolini ameuawa huko Italia.",
"NSDAP\nAdolf Hitler alijiunga na DAP mwaka 1919 kwa amri ya wakubwa wake jeshini. Wakati ule Hitler alikuwa bado mwanajeshi na wakubwa wake walitafuta habari juu ya vyama vingi vipya vilivyoundwa Munich baada ya mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Alionekana mara moja kama msemaji bora mwenye uwezo wa kuwahotubia wasikilizaji wake. Hotuba zake ziliwavuta watu wengi na chama kikamtegemea. 1921 Hitler alikuwa mwenyekiti wa chama.",
"Adolf Hitler\nTarehe 30 Aprili aligawa sumu kwa wote waliokuwa pamoja naye katika boma chini ya ardhi akawaruhusu kuondoka; aliagiza sumu ijaribishwe kwa mbwa wake mpendwa \"Blondi\". Mnamo saa 15.30 Eva Brau alijiua kwa kumeza sumu na Hitler alipigia risasi kichwani. Wasaidizi wa mwisho walibeba maiti hadi bustani ya ikulu na kuziweka katika shimo kutokana na mlipuko wa bomu; hapa wakazichoma kwa petroli.",
"Adolf Hitler\nBaadaye siasa ya kuwatenda Wayahudi vibaya na kuwaua katika maeneo fulani ilibadilishwa kulenga Wayahudi wote katika nchi zote zilizokuwa chini ya athira ya Ujerumani au kutekwa na jeshi lake. Hadi mwisho wa vita Wayahudi walikusanywa kutoka kote Ulaya na kupelekwa kwa reli hadi makambi ya mauti.",
"Adolf Hitler\nAlihutubia dharau na chuki ya kimbari dhidi ya watu wote wasio Wagermanik na hasa dhidi ya Wayahudi. Alisababisha Vita Kuu ya Pili ya Dunia na mateso ya watu milioni kadhaa. Akitangaza shabaha ya Ujerumani Mkubwa alisababisha kushindwa na kugawiwa kwa taifa lake pamoja na kupotewa na maeneo makubwa, hasa upande wa mashariki."
] | 35
|
Nani alizundua kifaa cha kupima joto?
|
[
"Kipimajoto\nUgunduzi wa kipimajoto umechangiwa na Galileo, ingawa aina ya kipimajoto kilichozibwa hakikuwepo mpaka mwaka 1650. Vipimajoto vya kisasa vinavyotumia spiriti na zebaki viliundwa na mjerumani Gabriel Fahrenheit ambaye pia alipendekeza kipimio cha jotoridi, kilichoitwa kwa jina lake - Fahrenheit, ambapo 32 F ni jotoridi la kuganda kwa maji na 212 F ni jotoridi la kuchemka kwa maji katika mkandamizo wa hewa wa kawaida. Vipimio vingi vilipendekezwa tangu muda wake. Katika kipimio cha centigrade au celsius, kilichobuniwa na mnajimu wa kiswideni Anders Celsius, ndicho kinachotumika sana dunia. Katika kipimio hiki maji huganda katika 0 C na huchemka katika 100 C."
] |
[
"Nani\nNani alikuwa mwanachama wa kawaida wa kikosi cha Kireno katika mechi za kufuzu kushiriki katika Euro 2008 UEFA, na alifunga bao moja kati ya mbili katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Ubelgiji tarehe 2 Juni 2007. Pia alimwandalia pasi safi mchezaji mwenzake Ricardo Quaresma aliyefunga bao katika mechi ya kirafiki dhidi ya Italia tarehe 6 Februari 2008. Fomu ya Nani kwa Manchester United wakati wa msimu wa 2007-08 hatimaye ilimwezesha kupata mwito kwa kikosi cha wachezaji 23 cha Luiz Felipe Scolari kwa ajili ya Euro 2008, pamoja na mchezaji mwenzake wa klabu Cristiano Ronaldo. Nadra alitumika katika kampeni hiyo, lakini aliweza kuanda pasi safi iliyomsababisha Helder Postiga kufunga bao baada ya kuingai katika dakika 15 za mwisho katika robo fainali dhidi ya Ujerumani tarehe 19 Juni 2008. Ureno hatimaye ilipoteza mechi hiyo 3-2.",
"Wabondei\nKama marehemu alikua ameoa ama kuolewa Linaandaliwa tambiko la kimila ambalo linaitwa kucha au mkucha ambapo mtu anachuku jembe na kikapu kisha panakokwa moto, mtu Yule anakwenda kujificha akishajificha anagonga lile jembe kidogo kisha anasema “Mkucha mkucha” mwengine anaitikia “Eehee” Yule mtu anasema tena “Fulani kafa” (Kwa kulitaja jina la aliekufa) Yule muitikiaji anauliza “Kafa?” kisha “kaolewa/kaoa wakati gani?” Yule mtu anautaja ule wakati “Wakati Fulani” Muitikiaji anauliza tena “Mahali kalipa?” atajibiwa kuwa amelipa ama hajalipa kisha watauliza madeni yake ya ndoa tu na atauliza pia alioa wake wangapi atajibiwa katika mfumo huo huo, ana watoto wangapi.. atajibiwa baada ya ukucha kumalizika sasa inafuata Ngoma ya Tindia na kisha Ngoma ya ukaa",
"Nanyindwa\nKijiji hiki ni maarufu kwa kutoa walimu wengi sana ambao walifundisha sehemu mbalimbali za wilaya ya Masasi, kama Carlo Mpupua, Richard Kandaya, Kamenya, Jacob Chitukoro aliyewahi kuwa msaidizi wa Katibu Mkuu wa CCM, Rashid Kawawa, Julius Savava, Luca Munlia, Walace Chitukuro, Brigita Fransis, Owen Lami na Charles Lami ambao walikuwa mapacha wakaacha kufundisha na kushangaza wengi, Pepetua na wengine wengi.",
"Joseph Kony\nJosph Kony alifikiriwa kuwa mtu mwenye pepo; amesawiriwa kama ama kma Masihi au shetani. Alizuru mara kadhaa milima ya Ato nchini Uganmda. Inadaiwa kuwa angekwea hadi kileleni cha milima na kulala huko kwenye jua kali kwa siku kadhaa. Angefunikwa na kundi la kumbikumbi wekundu ambao waliing'ata ngozi yake kwa undani. Mafuta kutoka mti uitwao Yao ilipakwa mwilini mwake. Kisha aliingia kwenye pango na kushinda huko pekee kwa majuma kadhaa. Alichowaamuru watoto wafanye kilikuwa kitu cha upuzi- aliwaambia kuwa iwapo wangechora mslaba kwenye vifua vyao na mafuta wangekingwa kutoka kutoka kwa risasi. Kony anasisitiza kwamba wanamugambo wa Lord's Resistance Army wanapigania Amri Kumi.\n\"Ndiyo, tunapigania Amri Kumi,\" Je, ni vibbaya? siyo kukiuka haki za binadamu. Na amri haikutolewa na Joseph. Haikutolewa na LRA. la, amri hiyo ilitolewa na Mungu. \"",
"Ondoa Giza Kitaa\nNari anaona watu wana mawazo ya kijinga kiasi kwamba hata lililo mbele yao wanashindwa kuliona. Anarejea maneno ya \"Macho Ngumu Kuona\". Uwoga katika maisha haukufanyi kufanikiwa bali kukudumaza. Sio kwamba ukiwa muoga ndio utaenda peponi. Namna ya ufundishaji ambao sio rafiki kwa wasomeshwaji. Watu hawaelewi kitu. Bado kuna wengine wanajifanya watumikia hip hop kumbe ndio wanafiki wakubwa katika suala zima la kuiponda. Wanashangazwa pamoja na majungu yao ndio kwanza muziki unapaa. Wanabaki na maswali tu. Vilevile anarejea jinsi Kilimo Kwanza kilivyoshindwa kumsaidia mtu wa hali ya chini. Nari anachukizwa na marafiki bandia wanajiofanya wanaeneza upendo ilhali wanaeneza skendo.",
"Nana Akufo-Addo\nMwishoni mwa utawala wa kijeshi wa Jerry Rawlings alianza tena kuandaa chama kipya cha NPP kuanzia mwaka 1992. \nKuanzia mwaka 1996 hadi 2008 alichaguliwa mara tatu kuwa mbunge. Mwaka 1998 alijaribu kuwa mgombea wa urais kwa niaba ya chama cha NPP lakini hakufaulu. Aliendelea kumfanyia kampeni mgombea mshindi John Kufuor. Baina ya 2001 na 2007 alikuwa waziri katika serikali ya rais huyo, kwanza kama waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu, halafu kama Waziri wa Mambo ya Nje ya Ghana.",
"Nonini\nBaadaye,wimbo Nani mwenza, kwa ushirikiano na mwanamuziki kutoka Tanzania Juma Nature, uliweza kujulikana kikanda. Katika ubunifu mkubwa hivi karibuni,ameshirikiana pamoja na msanii Nameless kuunda wimbo wa kitaifa wa Ijumaa ujulikanao kama \"furahi day\" ambao umechezwa sana katika vituo vya utangazaji. nyimbo zote mbili ziko kwenye albamu yake ya pili Mwisho Ya Mawazo,iliyotolewa mwaka 2007. Albamu yake iliwahusisha wanamuziki wakiwemo Nyota Ndogo, Mercy Myra, Profesa Jay na Q-Chief Agosti 2007, Nonini alikuwa miongoni mwa Wakenya 100 wenye ushawishi mkubwa kama ilivyochanguliwa na gazeti la The Standard Nonini alishinda tuzo bora la kimuziki la Chaguo La Teeniez mwaka 2008 kwa video yake ya \"Mtoto Mzuri\" katika Mwaka wa 2009 alitajwa kama Balozi wa international Lifestyle na Chuo Kikuu cha Limkokwing nchini Malaysia",
"Ashatu Kachwamba Kijaji\nAshatu Kachwamba Kijaji (amezaliwa 26 Aprili 1976) ni mwanasiasa Mtanzania na mwanachama wa Chama cha kisiasa cha Chama Cha Mapinduzi (CCM). Amechaguliwa kuwa mbunge wa Kondoa kwa miaka 2015 – 2020.",
"Nani\nNani husherehekea mabao yake kwa \"mfu\" au, kwa Kiingereza, \"mruko ya kifo\", sawa na ule wa Obafemi Martins na Lomana LuaLua. Njia hii ya kusheherekea, asili yake ni nyumbani anakotoka Nani katika \"capoeira\" , ambayo alikuwa anaifanyia mazoezi kama mtoto. Kwa muda, iliripotiwa kwamba meneja wa Manchester United, Alex Ferguson, alikuwa amempiga marufuku Nani kutosherehekea bao namna hiyo, kuogopea usalama wake, ingawa kamwe hii haikuungwa mkono na maneno yoyote ya moja kwa moja kutoka kwa Ferguson au Nani. Licha ya walidhani marufuku, Nani imeendelea kuadhimisha katika namna hii.",
"Nani\nNani aliuziwa Manchester United kwa kitita cha ada ambacho hakikutambuliwa, lakini linadhaniwa kuwa kati ya pauni (£) milioni 14 na 17, asilimia tano ambayo ililipwa kwa Real de Massamá. Alipasi matibabu yake tarehe 6 Juni 2007, na kusaini mkataba wa miaka mitano."
] | 24
|
Je, T-Pain alizaliwa lini?
|
[
"T-Pain\nFaheem Rasheed Najm (amezaliwa tar. 30 Septemba 1985) ni mwimbaji-mtunzi, rapa, na mtayarishaji wa rekodi kutoka nchini Marekani. Anafahamika zaidi kwa jina la kisanii kama T-Pain. Ameanza shughuli za urapa akiwa katika kundi la Nappy Headz. Mnamo mwaka wa 2005, akawa mwimbaji na kuweza kutoa albamu yake ya kwanza iliyoitwa \"Rappa Ternt Sanga\" ikiwa na vibao vyake vikali vya \"I'm Sprung\" na \"I'm N Luv (Wit A Stripper)\". Shughuli zake kama mwimbaji, T-Pain ametumia sana kionjo cha sauti cha Auto-Tune. Tangu kutolewa kwa albamu yake ya kwanza, T-Pain ametayarisha vibao kadhaa vikali vyake mwenyewe na vya marapa na waimbaji wengine wa R&B. T-Pain pia amekuwa na single kumi kwenye chati za Billboard Hot 100. Mnamo mwaka wa 2008, ameshinda tuzo ya Grammy na rapa Kanye West kwa ajili ya single ya \"Good Life\". Mnamo mwaka wa 2010 ameshinda tuzo nyingine ya Grammy na Jamie Foxx kwa ajili ya single ya \"Blame It\". T-Pain pia ni mwanzilishi wa studio ya kurekodia ya Nappy Boy Entertainment, imeanzishwa mwaka wa 2005."
] |
[
"I'm 'n Luv (Wit a Stripper)\n\"I'm 'n Luv (Wit a Stripper)\" (ilitambulika kama \"I'm 'n Luv (Wit a Dancer)\" au kwa kifupi \"I'm 'n Luv\") ni kibao kilichoimbwa na msanii wa R&B T-Pain akishirikiana na rapa Mike Jones. Imetolewa mwishoni mwa mwaka wa 2005 (ingawa muziki wake wa video haukutolewa mpaka wiki ya 16 Januari 2006), na kushika #5 kwenye chati za Billboard Hot 100, na kukifanya kuwa kibao cha pili cha T-Pain kuingia kwenye 10 bora, na cha kwanza kwa Mike Jones. Hiki ni kibao chenye mafanikio makubwa cha T-Pain mpaka sasa, kikafuatiwa na kibao chake kingine cha \"Bartender\", lakini kwa upande wa Mike Jones kimebaki kuwa hikihiki ndicho maarufu mpaka sasa.",
"U and Dat\n\"U and Dat\" ni kibao cha pili kutoka katika albamu ya E-40 \"My Ghetto Report Card\". Kibao kimemshirikisha msanii T-Pain na Kandi Burruss. Kibao kilitayarishwa na Lil Jon. Remix yake ilitolewa mwanzoni mwa mwezi wa Agosti na Juelz Santana, Snoop Dogg, na Lil Flip. Kibao hiki hupewa kete ya kwamba ndicho kilichompelekea T-Pain kuwa maarufu na kitikio bab-kubwa katika orodha ya nyimbo za hip hop zilizofanywa na T-Pain.",
"T-Pain\nNajm alizaliwa mjini Tallahassee, Florida. Jina lake la kisanii ni kifupi cha \"Tallahassee Pain\" (\"Tallahassee Mauimivu) na amechagua jina hilo kwa sababu ya ugumu wa maisha aliyoyapata wakati anaishi huko.",
"Plies\n\"The Real Testament\" ilitolewa mwezi Agosti 2007. Wimbo wake \"shawty\" akimshirikisha T-Pain ulishinda \"chati za\" nyimbo bopra za rapu na ilipata kushika nafasi ya tisa ya ngoma Motomoto 100. \"Hypnotized\", wimbo wa pili, ulioshirikisha Akon, na ilipata kushika nafasi ya tatu kwenye chati Rapu na 14 ya ngoma Motomoto 100. Wimbo wa kipekee wa tatu ulikuwa \"I Am The Club\". 29 Februari 2008, Kiwanda cha kurekodi cha Muungano wa Marekani/0} (RIAA) kuthibitishwa albamu imepita kiwango cha dhahabu kwa kuwa na kuuzwa zaidi ya mara 500,000 ; siku tano baadaye RIAA walifanya hivyo kwa ajili ya nyimbo \"shawty\" na \"Hypnotized\". Plies alifanywa mwimbjai mwalikwa katika wimbo wa kipekee wa Fat Joe \"Ain't Sayin' Nuthin\" kutoka \"The Elephant in the Room\" mapema mwaka 2008.",
"Rappa Ternt Sanga\nRappa Ternt Sanga ni albamu ya kwanza ya mtayarishaji/mwimbaji-mtunzi wa nyimbo za hip hop T-Pain, ilitolewa mnamo mwaka wa 2005. Jina la albamu ni lahaja ya matamshi ya rai \"rapper turned singer\", yaani, \"rapa aliyegeuka kuwa mwimbaji\". Albamu imeuza nakala zaidi ya 800,000 dunia nzima. T-Pain alikuwa na vibao viwili kwenye US Billboard Top Ten cha \"I'm Sprung\" na \"I'm 'n Luv (Wit a Stripper)\". Nyimbo nyingine kutoka katika albamu ni pamoja na \"I'm So High,\" wimbo unaohusu wa matumizi ya madawa ya kulevya. \"Rappa Ternt Sanga\" iliingia nafasi ya #40 kwenye Billboard 200 na ikaanguka nafasi hamsini hadi #91 juma lililofuata; majuma kadhaa ya usoni hatimaye ikapanda hadi nafasi ya #33. Moja ya nyimbo zilizobaki ni pamoja na \"You And Me\", toleo la awali la \"I Can't Wait\" la Akon. Albamu yote imetengenzwa na GarageBand.",
"Nelly Sachs\nNelly Leonie Sachs (10 Desemba 1891 – 12 Mei 1970) alikuwa mwandishi na mshairi Myahudi kutoka nchi ya Ujerumani. Mwaka wa 1940 alisaidiwa na rafiki yake Selma Lagerlof kukimbia ukatili wa WaNazi na kuhamia Sweden. Katika mashairi na tamthiliya zake alieleza mateso ya Wayahudi, k.m. katika tamthiliya \"Eli: Juu ya Mateso ya Israel\" (kwa Kijerumani \"Eli: Ein Mysterienspiel vom Leiden Israels\") iliyotolewa mwaka wa 1951. Mwaka wa 1966, pamoja na Shmuel Yosef Agnon alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.",
"Tundu Antiphas Mughwai Lissu\nMwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF anayetambuliwa na vyombo vya dola, Profesa Ibrahim Lipumba, naye ameonesha kukerwa na tukio la kutandikwa risasi kwa Lissu. Kwa uchungu, Lipumba amevitaka vyombo vya dola kuwatafuta wahusika wa tukio na wapelekwe katika vyombo vya sheria mara moja.",
"Tundu Antiphas Mughwai Lissu\nMnamo tarehe 7 Septemba 2017 majira ya saa saba mchana alipigwa risasi 38, lakini 16 tu katika hizo ndizo zilizompata katika sehemu za mkononi, miguuni na tumboni. Tukio hilo lilitokea nyumbani kwake Dodoma Area D. Baada ya kupata matibabu ya awali, Lissu alisafirishwa hadi jijini Nairobi kwa matibabu zaidi.",
"Ja Rule\nWakati wa miaka ya 2000, Ja Rule aliingia mkataba na The Inc. Records, ambayo awali ilikuwa ikitambulika kama Murder Inc. na ilikuwa ikiongozwa na Irv Gotti. Kutokana na vibao vyake na washirika wake, Ja Rule amepokea chaguzi nne za Grammy, na albamu zake sita zimeiingia katika kumi bora, mbili katika hizo ni \"\" (2000) na \"Pain Is Love\" (2001), imegonga vyema katika chati za US \"Billboard\" 200. Pia anafahamika sana katika jamii kwa kuwa na mgogoro na baadhi ya marapa wengine kama vile (hasa 50 Cent na Eminem)."
] | 42
|
Ukubwa wa Japani ni geographia ni kiasi gani?
|
[
"Japani\nNchi ina eneo la km² 377.944; na wakazi milioni 127; idadi hiyo imeanza kupungua."
] |
[
"Historia ya tarakilishi\nMwaka 1903, Ryōichi Yazu wa Japani aliiweka dhahiri Yazu Arithmometer. Hiki ni Kikokotoo analojia kilichotumia Mche Duara mmoja wenye gia ishirini na mbili (22), ambacho kilifanya hesabu mchanganyo katika mpango wa namba wa kizio cha pili na wa kizio cha tano. Hizi hesabu ni mashuhuri kwa watumiaji wa Soroban (Abakusi ya Kijapani).",
"Japani\nKijiolojia eneo hili liko kwenye mstari ambako mabamba ya gandunia ya Ulaya-Asia, Pasifiki na Ufilipino hukutana. Hii ni sababu ya kuwepo kwa volkeno 240 katika Japani na takriban 40 kati ya hizo ni hai pia kutokea kwa matetemeko ya ardhi ya mara kwa mara. Hivyo Japani ni sehemu ya pete la moto la Pasifiki linalozunguka bamba la Pasifiki.",
"Japani\nVisiwa vikubwa na muhimu zaidi ni vinne tu ndivyo Honshu, Hokkaido, Shikoku na Kyushu. Safu ya milima inapita visiwa vyote vikubwa na kusababisha msongamano mkubwa wa wakazi katika miji kutokana na uhaba wa ardhi ya kukalia. Hali halisi Japani yote ni safu ya milima tu inayopanda juu kutoka sakafu ya bahari na vilele vya milima yake huonekana juu ya uso wa bahari kama visiwa vikubwa au vidogo.",
"Wasuba (Kenya)\nMtegi ni mototo mwingine wa Girango, na walitoka Uganda sehemu ya Kitgum na wakatembea mpaka Karachuonyo. Na hapo walikaa kwa muda mrefu na wakahama mpaka nchi ya Wakipsigis. Na hapo walikaa sana, ndipo Tegi alipotengana na wenzake wakina Ongombe na Muruga. Na hapo ndipo Ongombe akahamia huko Kamagambo, ambapo hata hivi sasa bado wengi wao wanaishi huko na wanajulikana kama Wategi, \"ukoo wa Kamagambo\" au Kanyingombe. Wategi walianza kutelemka hadi wakafikia Kanyamkago na pale wakakaa kwa muda mrefu. Na kutokana na vita vya makabila walifukuzwa wakaja hadi Kanyamwa. Wategi walizidi kuja wengi kutoka huko nyuma walipokuwa wanabaki baki na wakajaa Nyandiwa na kuenea Mataro hadi Rasira Nyatambe. Mke wa Girango alikuwa binti wa Kijaluo kutoka Acholi na alizaa Gire kwao huko Kitgum–Uganda Kaskazini, kabla hajaolewa. Mke wa Girango alikuwa akiitwa \"Miluha\".",
"Japani\nWajapani wengi hukalia sehemu ndogo ya 10% za nchi. Kuna miji kumi yenye wakazi zaidi ya milioni moja. Miji mikubwa ni Tokyo, Yokohama, Nagoya, Osaka, Kyoto, Kobe, Hiroshima, Fukuoka, Kitakyushu, Sendai na Sapporo.\nUsafiri ndani ya Japani ni hasa kwa treni, mabasi na ndege. Treni ya Shinkansen visiwani Honshu na Kyushu ni kati ya treni zenye mkasi mkubwa duniani.",
"Jiografia ya Urusi\nTaiga ni kanda inayoenea kutoka mipaka ya magharibi hadi Pasifiki upande wa mashariki na kuwa 60% za eneo la Urusi kwa jumla. Inafunikwa kwa theluji kwa miezi mingi ya mwaka. Miti yake ni hasa aina mbalimbali za misonobari. Kutokana na baridi kuna wanyama wengi wenye manyoya mazito kama vile dubu, fisi-maji, melesi, elki, vicheche, wolverini na wengine waliovindwa kwa sababu ngozi zao zilitafutwa sana kwa matumizi ya koti katika nchi zote zenye majirabaridi kali. Uwindaji huu ulikuwa muhimu kiuchumi na sababu muhimu kwa uenezaji wa Urusi katika Siberia. \nMbuga baridi (kwa Kiingereza \"steppe\") ni kanda ya nchi inayoenea kuanzia Ukraina kupitia Urusi ya kusini hadi Kazakhstan na Manchuria. Uoto wake ni manyasi bila miti; miti inaweza kutokea penye maji karibu na mito au maziwa. Lakini kwa jumla tabianchi ya kanda hii ni yabisi au nusuyabisi ni hasa ukame unaozuia uoto wa miti.",
"Masai Mara\nHifadhi Mbuga ya Wanyamapori ya Kitaifa ya Masai Mara ina upana wa kilomita 1530 kieneo upande wa Kusini Magharibi mwa Kenya. Ndiyo sehemu ya Serengeti iliyo upande wa Kaskazini zaidi yenye upana wa jumla ya kilomita 25,000 kilomita kieneo. Upande wa Kusini imepakana na muga ya wanyama ya Serengeti, na upande wa magharibi na mharara wa Siria na upande wa Kaskazini Mashariki na Magharibi imepakana na maeneo ya ufugaji. Kiwango cha mvua katika mazingira haya huongezeka kuanzia kusini-mashariki-hadi magharibi, japo hubadilika kiwakati kutoka eneo moja hadi lingine na ni ya misimu miwili. Mito ya Sand, Talek na Mara ndiyo mito mikubwa ambayo hutoa maji kwenye hifadhi ya mbuga hii. Vichaka na miti iliyomea kwenye kingo za mito hufunika miteremko na vilele vya milima\nKimsingi mandhari ya hifadhi hii ni nyasi iliyowazi na mito. Eneo la Kusini Magharibi kuna vichka vya aina mbalimbli ya miti ya aina ya mwangate. Upande wa mpaka wa magharibi kuna harara(genge) la Esoit Oloololo la Bonde la Ufa, na wanyamapori wanapatikana eneo hili kwa wingi kwa sababu chemichemi ya maji hupatikana kwa urahisi na hakuna usumbufu wa watalii. Mwisho wa mpaka wa Mashariki ni kilomita 224 kutoka Nairobi, kwa hivyo, ni upande wa mashariki ndio hutembelewa na watalii sana.",
"Korea Kaskazini\nJeshi huwa na idadi kubwa ya vifaa lakini kuna tatizo kubwa la kwamba vifaru, ndege za kijeshi na manowari ni za kale sana na teknolojia ni ya miaka ya 1950-1970. Hakuna uhakika kiasi gani zinafanya kazi kutokana na hali bovu ya tasnia na uhaba wa vipuli. Korea Kaskazini ilijitahidi kutengeneza makombora na vifaa vingine kwa kunakili sampuli kutoka Urusi na China lakini inaonekana idadi iliyoweza kutengenezwa ni ndogo. Imekadiriwa na watazamaji kuwa wanaanga wanakosa mafuta ya kufanya mazoezi ya kutosha.",
"Tōgane, Chiba\nTōgane (東金市, \"Tōgane-shi\") ni mji wa Japani katika mkoa wa Chiba. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2003, mji una wakazi wapatao 61,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 58 kutoka juu ya usawa wa bahari. Eneo lake ni 89.34 km².",
"Go-Suzaku wa Japani\nGo-Suzaku (14 Desemba, 1009 – 7 Februari, 1045) alikuwa mfalme mkuu wa 69 (\"Tenno\") wa Japani. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa \"Atsunaga\", na alikuwa mwana wa Tenno Ichijo. Mwaka wa 1036 alimfuata kaka yake, Tenno Go-Ichijo, na kuwa mfalme hadi kujiuzulu mwaka wa 1045, siku mbili tu kabla ya kifo chake. Aliyemfuata kama Tenno ni mwana wake, Go-Reizei."
] | 60
|
Nchi ya Sudan ilipata uhuru mwaka gani?
|
[
"Sudan\nBaada ya uhuru wa nchi (1956), makabila ya kusini ambayo hayakukubali kusilimishwa yalipigania vita ndefu hadi kupata uhuru wao.",
"Sudan Kusini\nWakati wa uhuru wa Sudan mwaka 1956 viongozi wa kusini walidai haki ya kujitawala ndani ya taifa jipya, lakini mapatano yalishindikana na hali hiyo ilisababishwa kutokea kwa vita ya Anyanya kati ya 1956 na 1972.",
"Historia ya Sudan Kusini\nWakati wa uhuru wa Sudan mwaka 1956 viongozi wa kusini walidai haki ya kujitawala ndani ya taifa jipya, lakini mapatano yalishindikana na hali hiyo ilisababishwa kutokea kwa vita ya Anyanya kati ya 1956 na 1972."
] |
[
"John Garang\nSPLA ilipata msaada wa Libya, Uganda na Ethiopia. Garang na jeshi lake walidhibiti sehemu kubwa ya mikoa ya kusini mwa nchi, iliyoitwa \"Sudan Mpya\" . Yeye alidai kuwa 'ujasiri wa askari wake kutoka kwa \"uthibitisho kwamba sisi tunapambana vita vya haki. Hilo ni jambo ambalo Sudan Kaskazini na watu wake hawana. \" Wakosoaji walipendekeza motisha za fedha kwa uasi wake, wakibainisha kuwa kiasi kikubwa cha mafuta ya Sudan kiko katika kusini mwa nchi.\nGarang alikataa kushiriki katika serikali ya mpito mwaka wa 1985 au uchaguzi wa 1986, na kubaki akiwa kiongozi wa waasi. Hata hivyo, SPLA na serikali zilitia saini mkataba wa amani tarehe 9 Januari 2005 mjini Nairobi, Kenya. Tarehe 9 Julai 2005, aliapishwa kama makamu wa rais, cheo cha pili kwa ukuu katika nchi, kufuatia sherehe ambapo yeye na Rais Omar al-Bashir walitia saini katiba ya kugawana madaraka. Yeye pia alikuwa kiongozi wa utawala wa kusini mwa Sudan yenye uhuru mdogo kwa miaka sita kabla ya kufanyika kwa kura ya maoni ya uwezekano wa Kuganywa. Hakuna Mkristo au mtu kutoka kusini aliwahi kushikilia cheo cha juu kama hicho serikalini. Akizungumza baada ya sherehe, Garang alisema, \"Mimi nawapongeza watu wa Sudan, hii si amani yangu au amani ya al-Bashir, ni amani ya watu wa Sudan.\"",
"Historia ya Namibia\nMwaka 1978 Umoja wa Mataifa uliamua ya kwamba Afrika ya Kusini-Magharibi unapaswa kupewa uhuru. Baada ya miaka ya vita vya kupigania uhuru kati ya SWAPO na jeshi la Afrika Kusini, mchakato wa kimataifa wa kuelekea uhuru ulianza mwaka 1988 na hatimaye mwaka 1990 nchi ilipata uhuru wake kwa jina la Namibia.",
"Kura ya maoni ya uhuru wa Sudan Kusini, 2011\nKura ya maoni ilichukua nafasi Kusini mwa Sudan kuanzia tarehe 9 hadi 15 Januari 2011, katika hali ya aidha kanda ya kusini ibaki kuwa sehemu ya Sudan au iwe huru. Kura hii ya maoni ni moja kati ya tokeo la 2005 la Mkataba wa Naivasha baina ya Khartoum na serikali kuu ya Sudan People's Liberation Army/Movement (SPLA/M).",
"Mauaji ya kimbari\nMgogoro unaoendelea katika eneo la [[Darfur]], [[Sudan]], ambao ulianza mwaka wa 2003, ulitangazwa kuwa \"mauaji ya kimbari\" na Katibu wa Nchi ya [[Marekani]] [[Colin Powell]] tarehe 9 Septemba, mnamo mwaka wa 2004 katika ushahidi mbele ya [[Kamati ya Seneti ya Marekani ya Uhusiano wa Nje|Kamati ya Seneti ya Uhusiano wa Nje]]. Hata hivyo tangu wakati huo, hakuna mwanachama mwingine wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambaye ameufuata mfano huo. Kwa kweli, mnamo Januari mwaka wa 2005, Tume ya Kimataifa ya Uchunguzi wa Darfur, iliyoidhinishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Kimataifa Sheria nambari 1564 ya 2004, ilitoa taarifa kwa Katibu Mkuu ikisema kwamba \"Serikali ya Sudan haijafuata sera ya mauaji ya kimbari.\"",
"Sudan Kusini\nNchi imeathiriwa vibaya na vita vya kwanza vya Anya-nya (1) na vya pili Anya (2) na pia Vita vya Pili vya Wenyewe kwa Wenyewe vya Sudan vya SPLA / M kwa karibu miaka 21 tangu historia ya mwanzo wa SPLA / M mwaka wa 1983 - na kupelekea kutelekezwa vibaya, ukosefu wa miundomsingi ya maendeleo, na uharibifu mkubwa na kuhama kutoka makazi yao.",
"Namibia\nMwaka 1978 Umoja wa Mataifa uliamua ya kwamba Afrika ya Kusini-Magharibi unapaswa kupewa uhuru. Baada ya miaka ya vita vya kupigania uhuru kati ya SWAPO na jeshi la Afrika Kusini, mchakato wa kimataifa wa kuelekea uhuru ulianza mwaka 1988 na hatimaye mwaka 1990 nchi ilipata uhuru wake kwa jina la Namibia.",
"Historia ya Sudan Kusini\nNchi imeathiriwa vibaya na vita vya kwanza vya Anya-nya na vya pili Anya na pia Vita vya Pili vya Wenyewe kwa Wenyewe vya Sudan vya SPLA / M kwa karibu miaka 21 tangu historia ya mwanzo wa SPLA / M mwaka wa 1983 - na kupelekea kutelekezwa vibaya, ukosefu wa miundomsingi ya maendeleo, na uharibifu mkubwa na kuhama kutoka makazi yao.",
"Khartoum\nMwaka 2005 viongozi wa Sudan ya Kusini waliweza kufika Sudan baada ya mapatano ya amani kati ya serikali ya Khartoum na Jeshi la ukombozi wa Sudan Kusini. Walipewa vyeo mbalimbali katika serikali mpya. Baada ya kifo cha kiongozi wa Sudan ya Kusini John Garang katika ajali ya ndege palitokea ghasia kali mwanzo wa Agosti 2005.\nTangu mapatano ya amani kuhusu Sudan ya Kusini kuna mipango mikubwa ya kujenga kitovu kipya ya kibiashara kwa ajili ya Khartoum ni mradi wa \"Al-Mogran\". Kuna matumaini ya kwamba amani itawezesha nchi kutumia mapato kutokana na mafuta nchini kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Lakini wakati uleule vita ya jimbo la Darfur inaleta wasiwasi tena.",
"Mkimbizi\nTangu mwaka wa 2003, takriban wahamiaji 10,000 wasiokuwa Wayahudi kutoka nchi mbalimbali za Kiafrika wameingia nchini Israeli kinyume cha sheria. Takriban wakimbizi 600 kutoka kanda ya Darfur ya Sudan wamepewa hadhi ya ukimbizi. Wakimbizi wengine 2,000 kutokana na vita kati ya Eritrea na Ethiopia wamepewa ruhusa ya kuwa wakazi kwa muda kwa misingi ya kibinadamu. Nchi ya Israeli haipendi kuwatambua kama wakimbizi kwa hofu ya kuziaibisha nchi za Eritrea na Ethiopia. Wahamiaji waliosalia wanaishi nchini Israeli kinyume cha sheria. Mnamo mwaka wa 2007, Israeli iliwafukuza wakimbizi 48 hadi Misri baada ya wao kufanikiwa kuuvuka mpaka, ishirini kati yao walifukuzwa hadi nchi ya Sudan na serikali ya Misri, kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Msamaha. Mnamo mwezi Agosti mwaka wa 2008 Wanajeshi wa Ulinzi wa Israeli waliwafukuza nchini watafuta hifadhi wengine 91 wa Kiafrika mpakani. Katika kipindi chote cha mwaka huu, polisi wa Kimisri wamewapiga risasi na kuwauwa angalau watafuta hifadhi 20 wa Kiafrika waliokuwa wakijaribu kuingia Israel.",
"Sudan\nKhalifa alifaulu kupanua utawala wake juu ya maeneo karibu yote ya Sudan ya leo lakini alishindwa kufikia jimbo la Ikweta ambako Emin Pasha aliendelea kutetea mabaki ya Sudani ya Kimisri. \nItikadi ya kupanua utawala wa mahdiyya kwa njia ya jihad ilimsababisha khalifa kushambulia nchi jirani ya Ethiopia iliyotawaliwa na kaisari wa Kikristo. Mwaka 1887 akaongoza jeshi la askari 60,000 hadi Gondar. Waethiopia wakajibu kwa kushambulia Sudan mwaka 1889. Kifo cha Kaisari Yohane IV katika mapigano ya Metemma tarehe 9 Machi 1889 ililazimisha Waethiopia kurudi kwao. Lakini jeshi la mahdiyya lilipoteza wanajeshi wengi pia likadhoofika."
] | 18
|
Je, Jibuti ilipata uhuru mwaka upi?
|
[
"Jibuti\nNchi ilipata uhuru tarehe 27 Juni 1977.",
"Historia ya Afrika\nKatika mwaka wa 1977 Jibuti (Nchi ya Afars na Issas) iliyokuwa ikitawaliwa na Wafaransa ikarudi kwa wenyewe. Rhodesia (Zimbabwe) ikapata uhuru halisi mwaka wa 1980, na South West Africa, iliyokuwa ikitawaliwa na Afrika ya Kusini ikapata uhuru katika mwaka 1990 na kuitwa Namibia."
] |
[
"Uhuru Kenyatta\nKatika Novemba 2006 Biwott alirudia jaribio la kumpindua Uhuru kwa kuita mkutano wa Kanu mjini Mombasa bila idhini ya mwenyekiti wala kamati ya chama. Hapo alichaguliwa kuwa mweyekiti mpya. Kwa msaada wa serikali Biwott alifaulu kuandikisha kamati yake kama uongozi rasmi, na hivyo kumwondoa Uhuru katika nafasi ya kiongozi wa upinzani bungeni.",
"Historia ya Jibuti\nNchi ilipata uhuru tarehe 27 Juni 1977.",
"Uchumi wa Kenya\nMiaka kumi na tano ya Uhuru wa Kenya, kama ilivyokua miaka iliyopelekea uhuru, ilitawaliwa na sifa zilizomhusu Jomo Kenyatta miongoni mwa watu. Utawala wa Kenyatta uliofikia kikoma mnamo Agosti 1978, wakati kitabu hiki hakijakamilika, unaelezewa kwa ufasaha na. Kinaelezea mchango aliokuwanao Rais huyo katika muelekeo wa Kibepari (capitalist) na kijamaa (socialist) unaodhihirika katika mikakati ya kiuchumi nchini Kenya hivi sasa.\nUshawishi wa ari ya “kinyakuzi” enzi za Kenyatta ulikuwa na athari zake. Jomo Kenyatta, muasisi wa Taifa la Kenya atakumbukwa daima kwa mchango wake katika kupatikana kwa uhuru nchini mwake. Hata hivyo, inasemekana kuwa uhuru wa Kenya ulikuja na matatizo chungu mzima: Ukabila, Rushwa, na Choyo. Nafasi za kiutawala zilipatikana kwa wachache waliokuwa na madhumuni ya kukusanya Utajiri mkubwa kadiri iwezekanavyo. Hata hivyo, mtizamo huu wa jinsi hali ilivyokuwa, unakingana na jinsi hali halisi ilivyokuwa. Je? Hakukuwa na ukabila kabla ya uhuru? Kiukweli, Jomo Kenyata hakuwa muanzilishi, bali mdhibiti mkuu wa hali ya kikabila nchini humo. Ulikuwepo na bado upo japo kuwa unadhihirika katika ngazi fulani fulani. Miezi ya mwanzo ya utawala wa Rais Daniel Arap Moi, ilitawaliwa na bidii za dhati za kutaka kuondoa makosa yote yaliyojidhihirisha katika utawala uliotangulia na kwa bahati mbaya, ulikuwa ni wakati mbaya na mgumu kiuchumi nchini Kenya. Hata hivyo, mawazo ya kuwa matatizo yote yangeweza kuisha kufumba na kufumbua, yalikosa msingi pamoja na uzuri wa matokeo yaliyokusudiwa na kwamba ukabila na rushwa ambavyo hupatikana ulimwenguni kote, vingeweza kupotea. Ni rahisi sana kulaumu nyakati zilizopita kuwa ni sababu ya matatizo ya sasa na ni rahisi pia kufikiri kuwa mambo mazuri yanaweza kupatikana kwa haraka. Kukubali matatizo yaliyouandama uongozi wa Kenyatta, sio kukataa mazuri yalo ambatana nao. Hatua kubwa zilipigwa kimaendeleo ya jamii ya watu wa Kenya miaka kumi na tano baada ya uhuru, bila kuzingatia baadhi ya maandiko yanayoweza kuwa yameandikwa nchini Kenya na kitabu hiki, kinalenga kutoa ukweli na uhalisia wa mambo.",
"Uhuru Kenyatta\nUhuru Muigai Kenyatta (amezaliwa 26 Oktoba 1961) ni mwanasiasa nchini Kenya ambaye amekuwa rais wa nne na wa sasa wa Jamhuri ya Kenya. Baada ya kuongoza nchi, ameshinda uchaguzi mkuu wa Agosti 2017 lakini mahakama kuu ikaamua na kuamuru na kudai urudiwe, marudio ambayo licha ya kujiondoa kwa mpinzani wake mkuu Raila Odinga, Kenyatta aliibuka mshindi kwa asilimia tisini na nane. Hatimaye alitangazwa rasmi kuwa mshindi na kuapishwa kwa kipindi chake cha pili kwa mujibu wa sheria.",
"Chiwale\nKutokana na hali ya vita vya kupigania uhuru wakati huo nchini Msumbiji kati ya Wareno (wavamizi),na FRELIMO (wazalendo); kulitokea tatizo dhidi ya serikali ya Tanzania. Walitakiwa wahame kutokana na kuhofiwa usalama wao. Jumbe Habilu Limbende akatumwa kuwahamisha. Lakini mwenye Makolela alikataa na kusema maneno haya yafuatayo, \"MKITAKA MJE MNIUE HAPAHAPA NA FAMILIA YANGU, MIMI HAPA SIHAMI, KWANI PATAKUWA MJINI HATA NINYI WENYEJI MUTAHAMIA.\"\nNdipo jumbe Limbende akaondoka. Siku moja mwaka wa 1966, mzee Sandali alikwenda Nambaya (kijiji cha jirani na Chiwale), kutembea akakutana na mwalimu Barzolo Kambona ambaye ndiye alikuwa mwalimu wake wa shule ya msingi huko Mpeta Masasi. Nia ya safari ilikuwa ni kuonana na mwenye Chiwale. Hapo mzee Sandali akatumia fursa ya kuonana na mwalimu Barzolo kumuomba masomo ya kwanza/awali, chaki na mpira wa kuchezea wanafunzi ili aweze kuanzisha darasa la awali kama sehemu ya nyongeza ya masomo ya dini (Kur'an), ya Kiisilamu yaliyokuwa yakitolewa katika familia hiyo ya mwenye Makolela. Baada ya mwalimu Barzolo kumpatia vifaa hivyo aliweza kuanzisha darasa likiwa na watu wanane (8), miongoni mwao wasichana 5 na wavulana 3. Darasa hilo lilijengwa jirani na mwamba ulioko kando ya ziwa.",
"Wahehe\nHadi wakati huo, tayari von Heydebreck – mmoja wa manusura katika vita hivyo – alikuwa amekwishajeruhiwa na kuanguka akiwa amepoteza fahamu, lakini baadaye aliandika kwenye ripoti yake: “…Mfululizo wa matukio hadi wakati huu ulikuwa umetumia dakika mbili au tatu tu. Nilitambua hilo kabla ya kujeruhiwa, Wasudani tayari walikuwa wamekimbia kurudi nyuma vichakani baada ya kufyatua risasi mara mbili hivi. Mimi na askari wa Kikosi cha Tano tulilazimika kujilinda na kujitetea baada ya kuona Wahehe wakija katika umbali wa hatua 30. Kama sikosei, nilimsikia Sajini Tiedemann akisema alikuwa ameumia kabla hajafyatua risasi. Haikuwa rahisi kuona zaidi ya umbali wa hatua tano msituni kutoka pale njiani. Pia hakuna ambaye aliweza kunusurika kwa sababu Wahehe walikuja kwa kasi… Ni wazi walipanga kutushambulia baada ya kufika katikati msitu. Kuvurugika kwa mipango yao kulichangiwa hasa na kitendo cha Luteni von Zitewitz kufyatua risasi…”",
"Muziki wa Jibuti\nJibuti ni taifa dogo lipatikanalo katika Pembe ya Afrika ambayo imekuwa mitimdo mingi ya muziki za humo nchini. Watu wa huko wamejikidhi kwa wengi katika mji wa uvuo ambao pia huitwa Mji wa Jibuti.\nNchi hiyo imekuwa ikishirikishwa mataifa mengi, hivi maajuzi ikiwa Ufaransa. Jibuti ilikuwa nchi ya mwisho kupata uhuru kutoka Ufaransa.",
"Patrice Lumumba\nMaadhimisho ya uhuru wa Congo kwa mara ya kwanza yalifanyika mnamo tarehe 30 June 1960 ambapo maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na Mfarme Baudouinwa Ubeljiji pamoja na vyombo mbalimbali vya habari kutoka nchi za nje. Lumumba alitoa hotuba yake kama Waziri mkuu katika nchi huru japo yeye alikuwa ameenguliwa katika ratiba ya shughuli hiyo. Hotuba ya Mfalme wa Ubeljiji Mfalme Baudouin alihutubia kwa kutukuza utawala wa kikoloni, huku akilingania fikra za mjombae ambae alikuwa mfalme wa Ubeljiji akiitwa Léopold wa Pili glossing over atrocities committed during the Taifa huru la congo. Mfalme aliendelea kutoa masharti, \"aliwataka kuto kufanya mabadiliko yoyote mpaka hapo wao watakapo ona kwamba wanaweza kufanya vyema, na kwamba hawakutakiwa kufanya mabadiliko yoyote yalika bidhiwa na kwamba tutaendelea kutoa ushauri. \" Lumumba aliufahamisha umma kwamba uhuru uliotolewa na wabeljiji sio haukuja hivihivi:"
] | 18
|
Je,rais wa kwanza wa Marekani aliitwa nani?
|
[
"Orodha ya Marais wa Marekani\nKumeapishwa marais 43, na kumekuwa na marais 44, kwa sababu rais Grover Cleveland alihudumu mihula miwili isiyofuatana, na kwa hivi anahesabiwa mara mbili, kama rais nambari 22 na nambari 24. Marais wanne walifariki kawaida wakiwa mamlakani (William Henry Harrison, Zachary Taylor, Warren G. Harding, na Franklin D. Roosevelt), mmoja akajiuzulu (Richard Nixon), na wanne wakauawa (Abraham Lincoln, James A. Garfield, William McKinley, na John F. Kennedy). Rais wa kwanza wa Marekani alikuwa George Washington, aliyeapishwa 1789 bada ya kupigiwa kura na wajumbe wote katika kongamano. William Henry Harrison alihudumu kwa muda wa siku 31 pekee, mwaka 1841, naye Franklin D. Roosevelt akahudumu kwa muda mrefu zaidi kuliko wote, miaka 12. Rais wa sasa ni Barack Obama, aliyeapishwa 20 Januari 2009.",
"George Washington\nGeorge Washington (22 Februari 1732 - 14 Desemba 1799) alikuwa mwanasiasa, kiongozi wa kijeshi na rais wa kwanza wa Marekani kati ya 1789 na 1797."
] |
[
"Muna Lee (mwandishi)\nAkiwa kiongozi wa kupigania haki za wanawake, Muna Lee alifanya mchango muhimu katika harakati za kisasa za wanawake, hasa mapambano ya haki sawa. Alikuwa mwanzilishi wa Tume ya Wanawake ya Amerika Zote. Ilikuwa katika jiji la New York, alikokutana na mume wake wa baadaye, mshairi wa Puerto Rico na mwandishi wa habari aliyeitwa Luis Muñoz Marín, ambaye angekuwa gavana wa kwanza wa Pwetoriko wa kuchaguliwa kwa uchaguzi wa kidemokrasia. Walifunga ndoa mnamo tarehe 1 Julai 1919 na wakati wa muungano wao walikuwa na watoto wawili: binti mmoja Munoz Muna Lee (anayejulikana kama \"Munita\") na mwana mmoja Luis Munoz Lee. Muna alipewa talaka rasmi mnamo 15 Novemba 1946, miaka miwili kabla ya Luis Muñoz Marín kuandikwa katika vitabu vya historia alipochaguliwa kama gavana. Iwapo wangekuwa bado mume na mke, Lee angekuwa Mwanamke wa Kwanza wa kwanza wa kisiwa hicho cha Pwetoriko.",
"Joe Biden\nJoseph Robinette \"Joe\" Biden Jr. (amezaliwa 20 Novemba 1942) ni mwanasiasa wa Marekani. Kuanzia mwaka wa 1973 hadi 2009 alikuwa mbunge wa Senati ya Marekani akiwakilisha jimbo la Delaware. Halafu alikuwa Kaimu Rais wa Marekani chini ya Rais Barack Obama kuanzia mwaka wa 2009 hadi 2017, akiwa Mkatoliki wa kwanza na pia Mdelaware wa kwanza kuwa Kaimu Rais.",
"Vanessa Williams\nVanessa Lynn Williams (amezaliwa Machi 18, 1963) ni mwimbaji, mwigizaji, mtayarishaji, mwanamitindo wa zamani, na Mlimbwende wa Marekani kwa mwaka wa 1984 - kutoka nchini Marekani. Mwaka wa 1983, amekuwa Mwamerika-Mweusi wa kwanza mwanamke kupewa taji la Miss America. Juma saba kabla mwisho wa taji lake, lakini, kashfa ikatokea pale jarida la \"\"Penthouse\"\" liliponunua picha za utupu zisizoruhusiwa za Williams. Akavuliwa taji na kukabidhiwa mshindi wa pili wa taji hilo Bi. Suzette Charles wa New Jersey. Williams akarudi tena akiwa na kazi kama mburudishaji, na kupata teuzi kibao za Grammy, Emmy, na Tony Award. Mnamo September, 2015 katika shindano la Ulimbwende la America 2016, Afisa Mtendaji Mkuu wa Miss America Sam Haskell alimuomba radhi Williams (ambaye awali alisimama kama jaji mkuu) wa kulazimisha kujiuzuru kwake mnamo 1984.",
"Hubert Humphrey\nHubert Horatio Humphrey Jr. (27 Mei, 1911 – 13 Januari, 1978) alikuwa mwanasiasa wa Marekani. Kuanzia mwaka wa 1949 hadi 1964 alikuwa mbunge wa Senati ya Marekani akiwakilisha jimbo la Minnesota. Halafu alikuwa Kaimu Rais wa Marekani chini ya Rais Lyndon B. Johnson kuanzia mwaka wa 1965 hadi 1969. Mwaka wa 1968 aligombea urais yeye mwenyewe lakini akashindwa na Rais Richard Nixon. Kuanzia 1971 hadi kifo chake 1978 akawa seneta wa Minnesota tena.",
"Rais wa Marekani\nTangu marekebisho's ratificering, marais wanne kuwa aliwahi mbili Matokeo kamili: Dwight D. Eisenhower, Ronald Reagan, Bill Clinton na George W. Bush. Jimmy Carter na George HW Bush pili wakatafuta mrefu, lakini walikuwa na kushindwa. Richard Nixon alichaguliwa kwa muda ya pili, lakini alijiuzulu kabla ya kukamilisha hayo. Lyndon B. Johnson alikuwa rais tu chini ya marekebisho ukastahiki kumtumikia zaidi suala katika jumla mbili, baada ya kutumikia kwa miezi kumi tu zifuatazo John F. Kennedy 's kuuawa. Hata hivyo, Johnson kujiondoa kutoka 1968 Kidemokrasia ya Msingi, inashangaza Wamarekani wengi kwa kusema 'Mimi wala kutafuta, na mimi si kukubali, uteuzi wa chama wangu kwa muda mwingine kama rais wako'. Gerald Ford walitaka muda kamili, baada ya kutumikia nje miaka miwili iliyopita na miezi mitano ya pili ya Nixon mrefu, lakini hakuwa kuchaguliwa.",
"Robert Kennedy\nAlichaguliwa Mwanasheria Mkuu wa Marekani baada ya uchaguzi uliofanikiwa na aliwahi kuwa mshauri wa karibu zaidi kwa Rais kutoka 1961 hadi 1963. Umiliki wake unajulikana kwa utetezi wake kwa Movement ya Haki za Kiafrika na Marekani, kupambana na uhalifu uliopangwa na Mafia , na kuhusika katika sera ya kigeni ya Marekani kuhusiana na Cuba. Baada ya kuuawa kwa kaka yake, alibakia katika ofisi katika Utawala wa Johnson kwa miezi kadhaa. Aliondoka ili kukimbia Seneti ya Marekani kutoka New York mwaka wa 1964 na kushindwa na klabu ya Republican Kenneth Keating. Katika ofisi, Kennedy alipinga ubaguzi wa rangi na ushiriki wa U.S. katika vita vya Vietnam. Alikuwa mwanasheria wa masuala yanayohusiana na haki za binadamu na haki ya kijamii na kuunda uhusiano na Martin Luther King Jr. na Cesar Chavez.",
"Diana Ross\nMwaka wa 1976, jarida la \"Billboard\" wamemwita \"Mburudishaji wa Kike wa Karne.\" Mwaka wa 1993, kina \"Guinness Book of World Records\" wamemtangaza Diana Ross msanii wa kike mwenye mafanikio zaidi katika historia ya muziki akiwa na jumla vibao vikali 18 vikiwa nafasi ya kwanza huko nchini Marekani: 12 akiwa kama mwimbaji mkuu wa The Supremes na sita akiwa kama msanii wa kujitegemea. Ross alikuwa msanii wa kwanza mwanamke kushinda vibao vikali sita vikiwa nafasi ya kwanza. Ushirika huu unamweka nafasi ya tano katika wasanii wa kike wa kujitegemea kuwa na vibao vingi vya nafasi ya kwanza kwenyer Hot 100. Pia ni mmoja kati ya wasanii wachache wa rekodi kuwa na nyota mbili kwenye Hollywood Walk of Fame—moja akiwa kama msanii wa kujitegemea na nyingine akiwa kama mwanachama wa The Supremes. Mwezi wa Desemba 2007, amepokea Tuzo ya Heshima ya John F. Kennedy Center for the Performing Arts .",
"Kim Tae Jung\nKim Dae Jung (Kikorea: 김대중 金大中) (6 Januari 1925 - 18 Agosti 2009) alikuwa rais wa zamani wa nchi ya Korea Kusini. Mnamo mwaka wa 2000, amepata Tuzo ya Nobel ya Amani. Huyu ndiye mtu wa kwanza kutoka Korea kupata Tuzo ya Nobel.. Yeye ni Mroma tangu mwaka wa 1957, alikuwa kiitwa \"Nelson Mandela\" wa Asia . Kim Tae Jung alikuwa rais na aliyekuja kupokelewa na Kim Young-sam kuanzia mwaka wa 1998 hadi 2003. Alizaliwa mjini Haui-do, Mkoani South Jeolla, kisiwa kilichopo kwenye Pwani ya Korea Kusini.",
"George Washington\nTarehe 4 Februari 1789 alichaguliwa kuwa rais wa kwanza wa Marekani akirudishwa mwaka 1789. Baada ya kipindi chake cha pili alikataa kusimama tena akaunda hivyo utaratibu wa kwamba rais anaweza kurudishwa mara moja tu, hawezi kuendelea zaidi."
] | 56
|
Je,Uhispania ina idadi ya watu wangapi?
|
[
"Hispania\nEneo la nchi ni 500,000 km² ambalo lina wakazi wenye idadi zaidi ya watu milioni 44.395.286 (2006)."
] |
[
"Uislamu barani Amerika\nSuriname ina asilimia kubwa ya Waislamu katika ukanda huu, ikiwa na asilimia 13 au watu 66,307, kwa mujibu wa sensa yake ya mwaka wa 2004. Hata hivyo, Marekani, inakadiriwa kuwa na idadi kubwa licha ya kukosa sensa ya dini kwa Uislamu, ina aminika kuwa ina idadi kubwa ya Waislamu, kati ya milioni 1.3 na 2.7.",
"Mkimbizi\nKulingana na Agence France-Presse, Ujapani iliwakubali watu kumi tu kuingia nchini kama wakimbizi mnamo mwaka wa 2003, idadi ya watu ya chini kabisa nchi hiyo iliyowakubali kuingia nchini tangu mwaka wa 1997 ilipomkubali mtu mmoja pekee. Ijapokuwa iliwanyima hadhi ya ukimbizi, Ujapani iliwakubali watu 16 zaidi mwaka huo ikitumia misingi maalum ya kibinadamu - pia takwimu ya chini kabisa tangu mwaka wa 1997, ambapo iliwakubali watu watatu. Kwa kulinganisha, watu 336 waliomba kupewa hadhi ya ukimbizi nchini Ujapani mwaka huo, takwimu ya juu zaidi katika muda wa miaka miwili. Mashirika mbalimbali ya kimataifa, pamoja na Ubalozi wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, zimeomba nchi ya Ujapani kuwakubali wakimbizi zaidi.",
"Honduras\nWakazi walio wengi kabisa (90%) ni machotara hasa wenye asili ya mchanganyiko wa Waindio na Wazungu. Hao ndio asilimia 90 ya wakazi wote. Katika misitu ya milimani kuna bado vikundi vya wenyeji asilia (Wahindi wekundu, 7%). Wengine ni wa asili ya Afrika (2%) au ya Ulaya (1%) wasiochanganyika sana na wengine. Kwenye pwani ya kaskazini kuna makazi ya Wagarifuna ambao wana utamaduni wa mchanganyiko wa Wahindi wekundu na Waafrika.",
"Uhindi\nKwa eneo ina nafasi ya saba duniani, lakini kwa idadi ya wakazi (1,276,267,000 mwaka 2015) ni nchi ya pili baada ya China. Kati ya nchi za kidemokrasia ndiyo yenye watu wengi zaidi duniani. Tena inakadiriwa kwamba miaka ya hivi karibuni itapiku China.",
"Kanada\nMiji mingine mikubwa ni (idadi ya wakazi katika mabano):Wakazi asilia wa Kanada ni Waindio na Waeskimo. Walikuwa wameingia kutoka Siberia (Asia) Hakuna uhakika walikuwa wangapi wakati wa kufika kwa Wazungu lakini idadi yao ilipungua haraka kwa sababu watu kutoka Ulaya walileta magonjwa ya kuambukizwa na wenyeji walikosa kinga dhidi yake. Leo hii idadi imeongezeka tena kiasi: kuna takriban milioni 1.2 au asilimia 4.3 za Wakanada wote.",
"Amerika ya Kusini\nKijamii kulikuwa na matabaka. Tabaka la juu walikuwa Wahispania waliotumwa kutoka kwao pamoja na familia wenyeji Wahispania. Sehemu kubwa ya wakazi walikuwa na asili ya mchanganyiko wa Wazungu na Waindio; katika nchi kadhaa, hasa katika nyanda za juu za Andes na katika misitu ya mvua kulikuwa bado na idadi kubwa ya Waindio. Kwenye maeneo ya pwani watumwa kutoka Afrika waliingizwa. Serikali ya Kihispania ilijaribu kuwatenganisha wakazi kufutana na rangi na kutenga vyeo vya juu kwa Wazungu watupu, lakini hii ilikuwa vigumu kutokana na asilimia kubwa ya mchanganyiko.",
"Haiti\nWakazi asilia walikuwa Waindio Waarawak. Baada ya kufika kwa Kristoforo Kolumbus na utawala wa Hispania idadi yao ilipungua haraka kutokana na magonjwa ya Ulaya ambayo hawakuzoea na kukosa kinga dhidi yao na pia kutokana kutendewa vibaya kwa unyama na mabwana wapya. Mnamo mwaka 1600 Waindio wachache tu walibaki kutoka malakhi wakati wa Kolumbus wakapotea kabisa kwa njia ya kuoa au kuolewa na wazungu na weusi. Wahispania walianzisha mashamba kwa kazi ya watumwa kutoka Afrika.",
"Mkimbizi\nKolombia ina mojawapo ya idadi kubwa dunia ya watu waliokimbia makazi yao, na makadirio ni kati ya watu milioni 2.6 na 4.3, kutokana na mgogoro unaoendelea wa Kisilaha wa Kolombia. Takwimu ya upeo wa juu ni ya kuongeza idadi ya wakimbizi tangu mwaka wa 1985. Hivi sasa inakadiriwa na [Kamati ya Wakimbizi na Wahamiaji ya Marekani] kwamba kuna Wakolombia 150,000 katika \"hali kama za ukimbizi\" nchini Marekani, wasiotambulika kama wakimbizi au wasiopewa ulinzi wowote rasmi.",
"Guyana ya Kifaransa\nWakazi walio wengi ni wa asili ya Afrika au wa mchanganyiko wa Kiafrika-Kizungu (60-70%). Asilimia 14 ni Wazungu; wengine ni Waindio asilia (3-4%), Wachina (3-4%), Wahindi na wahamiaji wa hivi karibuni kutoka Laos (1-2%).",
"Wilaya ya Laikipia\nWakikuyu walikuwa takribani 60% ya idadi ya watu wote kwenye wilaya hii, huku idadi iliyosalia ikijumuisha watu wa makabila mengine, ni pamoja na Mukogodo Masai, Wasamburu, Wameru, Waborana, Wakalenjin, Wasomali, Wazungu, Watu wa asili ya Asia, na Waturkana, wakiipa wilaya hii idadi ya watu tofauti tofauti. Mashamba mengi yanamilikiwa na idadi ndogo ya masetla wa ukoloni."
] | 31
|
Mbegu ya maharagwe iko na asili gani?
|
[
"Mharagwe-pana\nMharagwe-pana (\"Vicia faba\") ni jina la mmea katika familia Fabaceae. Mbegu zake huitwa maharagwe mapana. Asili ya mmea huu ni Mashariki ya Kati lakini siku hizi hukuzwa mahali poti katika kanda za nusutropiki na wastani. Vipande vinavyolika ni mbegu (bichi na bivu), matumba machanga na majani.",
"Maharagwe\nMharagwe ni mmea ukuao kwa mwaka mmoja wenye asili ya Amerika ya Kati ya kale na huko Andes, na sasa unalimwa maeneo mengi duniani kwa mbegu zake za maharagwe zinazoliwa, zilizo maarufu zote zikiwa zimeiva na hata zikiwa bado mbichi. Tani milioni 18.3 za maharagwe makavu na nyingine milioni 6.6 za maharagwe mabichi zililimwa mnamo mwaka 2007 duniani kote. Maharagwe ni miongoni mwa vyakula vikuu vya huko Amerika."
] |
[
"Wasuba (Kenya)\nMtegi ni mototo mwingine wa Girango, na walitoka Uganda sehemu ya Kitgum na wakatembea mpaka Karachuonyo. Na hapo walikaa kwa muda mrefu na wakahama mpaka nchi ya Wakipsigis. Na hapo walikaa sana, ndipo Tegi alipotengana na wenzake wakina Ongombe na Muruga. Na hapo ndipo Ongombe akahamia huko Kamagambo, ambapo hata hivi sasa bado wengi wao wanaishi huko na wanajulikana kama Wategi, \"ukoo wa Kamagambo\" au Kanyingombe. Wategi walianza kutelemka hadi wakafikia Kanyamkago na pale wakakaa kwa muda mrefu. Na kutokana na vita vya makabila walifukuzwa wakaja hadi Kanyamwa. Wategi walizidi kuja wengi kutoka huko nyuma walipokuwa wanabaki baki na wakajaa Nyandiwa na kuenea Mataro hadi Rasira Nyatambe. Mke wa Girango alikuwa binti wa Kijaluo kutoka Acholi na alizaa Gire kwao huko Kitgum–Uganda Kaskazini, kabla hajaolewa. Mke wa Girango alikuwa akiitwa \"Miluha\".",
"Ngai\nKama ilivyo katika makabila mengineo ya Afrika Ngai hutolewa kafara, ni muumba, anauwezo dhidi ya viumbe na hata vitu visivyo kuwa na uhai na kadhalika. makazi yake kulingana na hadithi ya asili ya Agikuyu ni mlima Kenya (Kirinyaga). Kulingana na hadithi hii, Ngai alimuumba Gikuyu na mkewe Muumbi. Akawapa eneo la Muranga kama makazi yao. Akawabariki na mabinti tisa, kisha akaumba vijana tisa wa kiume iliwawaoe walipobaleghe. Kizazi baada ya kizazi jamii ya wakikuyu ilichipuka kutoka kwa nyumba hizi tisa. Majina ya Nyumba hizi hufanana na yale ya mabinti wa Gikuyu.",
"Maharagwe\nHuko Meksiko, Amerika ya Kati na Amerika ya Kusini, chakula cha asili cha maharagwe ni epazote, ambacho husemekana kuongeza mmeng’enyo wa chakula.",
"Maharagwe\nAina nyingine ya maharagwe ni haragwe pana, mbegu ya \"Vicia faba\", ambayo tani milioni 3.7 tu zililimwa mwaka 2007. Biashara ya maharagwe imejigawanya vizuri katika nchi za Asia, Afrika, Ulaya, Oceania, Amerika ya Kusini na Amerika ya Kaskazini. Brazili ndiyo wazalishaji wakuu wa maharagwe makavu huku China wakiwa ndiyo wazalishaji wakuu wa maharagwe mabichi, kwa wastani sawa na wazalishaji kumi wote waliobakia kwa pamoja.",
"Wagadugu\nMji ni pia kitovu cha usafiri na mawasiliano. Kuna kiwanja cha kimataifa cha ndege na njia ya reli kwenda Abidjan (Côte d'Ivoire), halafu barabara za kwenda Lome (Togo), Bamako (Mali), Niamey (Niger), Accra (Ghana).",
"Kenya\nKwa upande wa mbio za magari, Kenya ndio waandalizi wa mbio za magari maarufu za Safari Rally zinazotambulika kuwa ngumu zaidi ulimwenguni, na ambazo ni sehemu ya Bingwa wa Mbio za Magari kwa miaka mingi hadi kuondolewa kwake baada ya mbio za 2002 kwa sababu ya matatizo ya kifedha. Baadhi ya madereva maarufu wa mbio za magari ulimwenguni walioshiriki na kushinda mbio hizi ni Bjorn Waldegard, Hannu Mokkola, Tommi Makinen, Shekhar Mehta, Carlos Sainz na Colin McRae. Ingawa mbio hizi bado huendelea kila mwaka kama sehemu ya kutafuta Bingwa wa Mbio za Magari Afrika, waandalizi wanatarajia kuruhusiwa kujiunga tena na Ubingwa wa Magari Ulimwenguni katika miaka michache ijayo.",
"Mahindi\nMbegu za mahindi huwa na sehemu ya nje iliyoungana na gamba la nje la mbegu, kama ilivyo kawaida kwa mimea mingi ya jamii ya nyasi. Muhindi huwa na mbegu nyingi, ambazo huwa hazuungani hata maramoja , na nkila moja ikiwa na ukubwa wa kama njegere hivi, zikiwa zimejipanga kwenye mistari kuzunguka gunzi ambamo zimejishikiza. Gunzi moja huweza kuwa na punje za mahindi takribanui 200 – 400, na huwa na urefu wa sentimita 10 -25. Pia huwa na rangi mbalimbali: nyeusi, kijivu, nyekundu, hudhurungi, nyeupe na njano. Zinaposagwa kuwa unga, unga wa mahindi hupatikana kwa kiasi kikubwa, huku ukiwa na makapi kidogo kuliko ngano. Lakini unga wa mahindi huwa unakosa protini muhimu ya ngano, na hivyo, kufanya uokaji kushindwa kuwa na uwezo mkubwa wa kuumuka na kufanana.",
"Wapare\nHata hivyo Wapare wa Mwanga wamegawanyika katika jamii mbili: Wasangi na Wagweno. Wakati Wasangi anaongea Kipare kinachoongelewa pia na Wapare wa maeneo mengine, Wagweno wao wana lugha yao iitwayo Kigweno. Kigweno ni mchanganyiko wa Kipare na Kichagga. Hii inaonesha kuwa asili ya Wagweno ni Uchagani, japo zipo nadharia kadha wa kadha zinazoeleza asili ya Wagweno kuwa huenda hata hawana asili ya Uchaga wala Upare lakini mbali na uhusiano wa lugha kinachofanya waonekane kuwa ni sehemu ya Wapare ni namna tamaduni zao nyingine zinavyofanana na Wapare, pia kuchanganyika katika maisha ya kila siku kwenye milima ya Wapare pamoja na Wagweno wengine kuwa na majina ya koo zinazofanana na za Wapare kama Wasuya na Wavungi. Hata hivyo mila na desturi nyingi za Wagweno zinafanana zaidi na zile za Wapare wengine."
] | 52
|
Mtandao wa Youtube ulianzishwa na nani?
|
[
"YouTube\nYouTube ni tovuti ya kushirikisha video ambazo watumiaji wanaweza kuzinakili na kuzigawa kwa wengine. Wafanyakazi watatu wa zamani wa PayPal waliunda YouTube mnamo Februari 2005."
] |
[
"Mtandao wa kompyuta\nWavuti za ndani na wavuti za nje zinaweza au zisiweze kuwa na uhusiano na Mtandao. Ikiwa zimeunganishwa na mtandao, wavuti za ndani na wavuti za nje kwa kawaida hupewa ulinzi dhidi ya kutumiwa kutoka kwa wavuti bila ruhusa ifaayo. Mtandao hauchukuliwi kuwa sehemu ya wavuti wa ndani na wavuti wa nje, ingawa inaweza kutumika kama vipengele vya kutumia sehemu za wavuti za nje.",
"Ondoa Giza Kitaa\nNari anaona watu wana mawazo ya kijinga kiasi kwamba hata lililo mbele yao wanashindwa kuliona. Anarejea maneno ya \"Macho Ngumu Kuona\". Uwoga katika maisha haukufanyi kufanikiwa bali kukudumaza. Sio kwamba ukiwa muoga ndio utaenda peponi. Namna ya ufundishaji ambao sio rafiki kwa wasomeshwaji. Watu hawaelewi kitu. Bado kuna wengine wanajifanya watumikia hip hop kumbe ndio wanafiki wakubwa katika suala zima la kuiponda. Wanashangazwa pamoja na majungu yao ndio kwanza muziki unapaa. Wanabaki na maswali tu. Vilevile anarejea jinsi Kilimo Kwanza kilivyoshindwa kumsaidia mtu wa hali ya chini. Nari anachukizwa na marafiki bandia wanajiofanya wanaeneza upendo ilhali wanaeneza skendo.",
"Nonini\nBaadaye,wimbo Nani mwenza, kwa ushirikiano na mwanamuziki kutoka Tanzania Juma Nature, uliweza kujulikana kikanda. Katika ubunifu mkubwa hivi karibuni,ameshirikiana pamoja na msanii Nameless kuunda wimbo wa kitaifa wa Ijumaa ujulikanao kama \"furahi day\" ambao umechezwa sana katika vituo vya utangazaji. nyimbo zote mbili ziko kwenye albamu yake ya pili Mwisho Ya Mawazo,iliyotolewa mwaka 2007. Albamu yake iliwahusisha wanamuziki wakiwemo Nyota Ndogo, Mercy Myra, Profesa Jay na Q-Chief Agosti 2007, Nonini alikuwa miongoni mwa Wakenya 100 wenye ushawishi mkubwa kama ilivyochanguliwa na gazeti la The Standard Nonini alishinda tuzo bora la kimuziki la Chaguo La Teeniez mwaka 2008 kwa video yake ya \"Mtoto Mzuri\" katika Mwaka wa 2009 alitajwa kama Balozi wa international Lifestyle na Chuo Kikuu cha Limkokwing nchini Malaysia",
"David Mathayo David\nMwanzo wa siasa\nSiasa alizianza rasmi mwaka 1995 alitumia TV yake kwenda kuonyesha vijijini madhara ya vyama vingi, alitumia mapigano ya Rwanda na Burundi kama kutishia wananchi wasikubali upinzani na kipindi kile wananchi walikuwa wepesi kuelewa kumbuka TV hazikuwa nyingi Tanzania kipindi kile. Alijijengea umaarufu sana ndani ya chama mkoani Morogoro na kitaifa. Aligombea ujumbe wa NEC mkoa wa Morogoro kundi la vijana alishinda. Mathayo alimaliza SUA 1997 na kupata kazi ya kufundisha chuo kimoja huko Serowe Botswana. Kwa kuwa mjumbe wa NEC alikuwa karibu na akina Lowasa, JK na vingunge wengine aliweza kuwa anaonana na akina Makamba na akawa ni mwanamtandao. Wakati huo Matayo alikuwa akirudi Tanzania kufanya shughuli zake za kisiasa wakati bado ni mwajiriwa wa serikali ya Botswana. Kwa mfano wakati mmoja alirudi Tanzania na kuwahamasisha wanafunzi wa SUA (kama 200 hivi) na kuwapeleka Dodoma kupokea kadi za CCM chini ya mwenyekiti wa CCM Mkapa. Wanafunzi walahidiwa wangepatiwa ajira kwa kufanya hivyo. Hii ilimjenga sana Matayo ambaye aliisha kuwa maarufu kwenye ofisi za chama Dodoma, kama mjumbe wa NEC na mkutano mkuu. Mwaka 2000 aligombea Ubunge Same Magharibi na kushinda na kuteuliwa kuwa waziri mdogo. Wakti huu aliisha tamka kwamba amesomea Afrika Kusini digrii ya falsafa (PhD). Prof Msolla wakati aliyekuwa waziri wa elimu ya juu na sayansi ambaye aliwahi kufundisha SUA alimjua sana Matayo na alimwita Matayo na kumuuliza kuwa PhD alifanya lini na wapi na pia aletee PhD thesis yake. Prof Msolla alisema \"Matayo aliogopa sana na alikili mbele yangu, kuwa Prof mimi nimetumia hii title kisiasa zaidi, sina MSc wala PhD”.",
"SHIWATA\nSHIWATA ni Mtandao wa Wasasnii Tanzania. SHIWATA awali ilijulikana kama \"SHIRIKISHO LA WASANII TANZANIA\", bali kutokana na mgongano wa usajili na Msajili ambae ni Baraza la Sanaa la Taifa baadae ilikubalika kwamba iitwe Mtandao wa Wasanii kutokana na Kusajiliwa kwa mashirikisho manne \"Shirikisho la Wasanii Tanzania \" pamoja na kubadilishwa kuwa Mtandao wa Wasanii limeendela kuitwa \"SHIWATA\".\nSHIWATA ni mtandao wa wasanii Tanzania ambao ulianzishwa mwaka 2002 kwa lengo la kuwaweka pamoja Wasanii, wanamichezo na wanahabari. Mkusanyiko huu wa wasanii mbalimbal;I ndio uliopelekea kuanzisha umoja ambao kwa sasa umeandaliwa kama chombo cha kuwaweka pamoja wadau wote walio katika tasnia za Sanaa, Michezo na Habari kwa kupewa eneo la kujenga nyumba zao za kuishi na tayari mradi huo umeshaanza kutekelezeka kwa baadhi ya wasanii kujenga nyumba ambapo wenginee wameshahamia tayari katika kijiji cha Wasanii kilichopo Mwanzega wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani \nHii ni orodha ya baadhi ya wasanii maarufu kutoka katika makundi mbalimbali kama yalivyo ainishwa hapa chini kuzingatia makundi ya kitasnia kwa ushahidi zaidi unaweza kuona katika blog ya SHIWATA.\n(English)",
"Ghosts (video)\nMilango mikubwa miwili ilifunguka na kubainika kuwa ni mikubwa sana, ndani kiza kinene kwenye ukumbi. Kwa kusita, wanakijiji wale wakawa wanaeleka wenyewe kwenye eneo la ukumbi wa kuchezea, ambapo walisalimiwa na Bwana mchawi ambaye alikuwa bado anawatisha na vimadawa vya moshi pale pa kuingilia. Meya akawa na jazba naye na kumfanyia fujo, na kuthubutu kumwita yule Mchawi \"kumbe cha ajabu\", \"kituko\", na \"anatisha\", na kumweleza kwamba hakaribishwi kabisa katika mji wao. Yule mchawi akaanza kujitetea, na kujibu vitisho vya Meya kwamba \"Utaondoka mwenyewe, ama unataka nikujeruhi?\" (Watu wa mjini pale wakaonekana wanataka kujiharishia, lakini hawakuruhusiwa kutoa pingamizi).",
"Nandy\nMwanzoni mwa mwaka wa 2016 alishiriki kwenye mashindano ya kuimba yaliyoandaliwa na \"Tecno\". Shindano lilishirikisha washiriki wengine kutoka nchi kibao za Afrika na kipindi cha fainali kilichofanyika huko Lagos, Nigeria, Nandy aliibuka kama mshindi wa pili. Shindano hili lilimkuza kimuziki, hasa katika suala zima la utumbuizaji jukwaani, alipata maarifa ya ya muhimu kutoka kwa makungwi wa muziki kama vile akina M.I Abaga, Yemi Alade na Bien wa Sauti Sol.",
"Chocheeni Kuni\nNatoa katoni ishirini za sabuni ya unga, aliyekwambia wale wachafu nani?\nKasafisheni kwanza nyoyo zenu ndio mrudi kwa wananchi\nNdugu zangu, tawi kavu, kuanguka wala sio ajabu\nWakati wao wanatenganisha mavi ya panya kwenye unga\nNinyi chicheeni kuni zilizoloa, maji yapate moto ugali usongwe\nwakiwauliza, waambieni huu ni utani hehehe, Hapa kwetu tuna makabila 120, tunataniana\nWaliopo hatuwataki, wanaotaka hatuwaamini\nManeno siku zote yanauma na yanachefua ukijua maana yake\nKwa mfano neno la kitoto, mtoto kumwambia mtoto tunasema watoto wanacheza\nNeno la kitoto, mtoto kumwambia mkubwa tunasema mtoto anakuwa\nMtoto akisema babaa, ile ndege yangu,\nBaba hata kama huna baiskeli, utamwambia ikitua nitakuletea, ndio utaratibu\nLakini maneno ya kitoto, mtu mzima kumwambia mtu mzima mwenzie, kuna walakini\nMimi safari imenishinda, na sitaki tena kuulizwa kwanini",
"Dom Down Click\nBaada ya makutano ya mara kadhaa, likaja suala la kwenda kurekodi ndipo sasa baadhi ya marafiki wa pale kitaa wakajitokeza kama na kujulikana kama nao waghanaji. Watu hao waliojitokeza baada ya azimio la kwenda studio ni pamoja na Adam Shule Kongwe, Dilema Bonito, Goda, Badi, K2da, na Andre K. wote wakiwa chachu kubwa kuazisha hizi harakati kwa pamoja wakakubaliana waende kurekodi na wakafanikiwa kurekodi wimbo wa kwanza uliyokwenda kwa jina la \"Usika wa Manane\". Kwa bahati mbaya, wimbo huo haujafanikiwa kutolewa. Baada ya kufanikisha ngoma ya kwanza, uraibu wa kurekodi wimbo mwingine zaidi ukawajia. Ikawa kawaida sasa kila Jumapili kwenda studio na kuanza kurekodi ngoma mbalimbali kwa kutumia biti za mbele. Baada ya kurekodi nyimbo kibao, wakaona sasa inafaa sasa kuachia ngoma kutoka katika kundi, ndipo walipotoa \"Fikra za Wazawa\" ambayo ndani yake kulikuwa na Badi, Kagusa, Koku, SlimSal. Ili kuandaa ngoma hii ilibidi watumie biti la Duke ambalo walilitumia bila idhini yake. Biti hilo walilichukua katika mafaili ya Nash MC wakati huo alivyoenda Dodoma. Biti hilo hajachukua idhini ya Nash wala Duke.",
"Soko la Hisa la Nairobi\nOfisi na sakafu ya biashara za NSE ziko katika jumba la Nation Centre katika baraste ya Kimathi. Biashara hufanywa kupitia Electronic Trading System (ETS) ambayo ilikamilika mwaka wa 2006. Mtandao wa Wide Area Network (WAN) uliwekwa mwaka wa 2007 na hili lilitupilia mbali haja ya Kampuni za kuuza na kununlia Hisa kuwapeleka mawakala wao (wafanyabiashara) kwenye ukumbi wa biashara ili kuuza au kununua hisa. Kwa sasa, shughuli za kununua na kuuza hufanywa kutoka ofisi zao kupitia mtandao wa WAN. Hata hivyo, baadhi ya mawakala bado wanaweza kufanya biashara kutoka sakafu ya NSE."
] | 2
|
Je,Günter Wilhelm Grass alishinda tuzo la Nobel mwaka upi?
|
[
"Günter Grass\nGünter Wilhelm Grass (alizaliwa 16 Oktoba 1927 Danzig, alifariki 13 Aprili 2015 mjini Lübeck) alikuwa mchoraji, mchongaji na mwandishi kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa ameandika riwaya na insha, na pia tamthiliya na mashairi. Mwaka wa 1999 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.",
"Günter Grass\nAlipokabidhiwa Tuzo ya Nobel ya Fasihi mwaka 1999 taasisi ya taaluma ya Sweden ilieleza: \"Katika 'Ngoma ya Bati' Grass alichunguza historia ya kisasa kwa kukumbuka wale waliosahauliwa, wahanga na ule uwongo ambao watu wanataka kusahau kwa sababu waliwahi kuuamini\"."
] |
[
"Günter Grass\n1954 alifunga ndoa na Mswisi Anna Schwarz akaishi naye Paris, Ufaransa kati ya 1956 hadi 1960. Alizaa naye watoto wanne wakaachana 1972 na kuwa na talaka ya mwaka 1978. Baada ya kuaachana na Anna akawa na uhusiano wa kimapenzi na Veronika Schröter halafu Ingrid Kruger akazaa watoto nao pia. 1979 alimwoa Ute Grunert akakaa naye hadi mwisho. Wakati wa kifo chake alikuwa na wajukuu 18.",
"Günter Grass\nWakati wa kukaa Paris alitunga muswada wa riwaya yake ya kwanza \"Die Blechtrommel\" (ngoma ya bati) iliyompatia umaarufu mara ya kwanza katika Ujerumani. Katika riwaya hii sawa na vitabu vyake vilivyofuata alisimulia habari za Wajerumani wakati wa vita na chini ya utawala wa chama cha Nazi cha Adolf Hitler. Alijadili hapa swali la hatia ya Wajerumani kwa jinai zilizotendewa chini ya mfumo wa siasa ya miaka ya Hitler.",
"Günter Grass\nRiwaya za \"Katz und Maus\" (Paka na panya) na \"Hundejahre\" (miaka ya mbwa) zilifuata 1961 na 1963. Zote tatu zinasimulia maisha ya watu kutoka mji wake Danzig ambayo tangu 1945 imekuwa mji wa Poland ilhali wakazi wote Wajerumani walifukuzwa. Maandiko ya Grass yalisababisha majadiliano makali katika jamii ya Ujerumani juu ya historia ya taifa na swali la hatia ya kuvumilia na kushiriki katika mfumo wa kisiasa ya miaka ya Hitler.",
"Wilhelm Conrad Röntgen\nWilhelm Conrad Röntgen (27 Machi 1845 – 10 Februari 1923) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa anajulikana kwa ugunduaji wa mionzi ya eksirei. Mwaka wa 1901 alikuwa mshindi wa kwanza wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.",
"Günter Grass\nGrass alizaliwa katika dola-mji Danzig (leo Gdansk, Poland) akiwa mwana wa mfanyabiashara Mjerumani na mke wa asili ya Kashubi. Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia alijitolea kuwa mwanajeshi Mjerumani akiwa na umri wa miaka 15 na kwa umri wa miaka 17 alikuwa mwanajeshi wa kiosi cha SS.",
"Assia Djebar\nMnamo mwaka wa 1996, Djebar alishinda tuzo maarufu la Kimataifa la Neustadt la Fasihikwa mchango aliofanyia fasihi Duniani. Mwaka uliofuata, alipeleka nyumbani Tuzo la Yourcenar. Djebar pia amependekezwa mara nyingi kwa tuzo la la Nobel la Fasihi.\n« Immortelle » Éditorial. In : Le Monde, Samedi 18 juin 2005, p 17",
"Frederick Duncan Michael Haldane\nFrederick Duncan Michael Haldane (amezaliwa 14 Septemba, 1951) ni mwanafizikia kutoka nchi ya Uingereza. Mwaka wa 2016, pamoja na David James Thouless na John Michael Kosterlitz, alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Alipewa tuzo kwa utafiti wa kinadharia katika maelezo ya tabia za mata katika hali karibu na sifuri halisi (ing. \"\"for theoretical discoveries of topological phase transitions and topological phases of matter\"\")\nProfesa John Chalker, mkuu wa idara ya Fizikia ya Kinadharia kwenye Chuo Kikuu cha Oxford anajaribu kueleza tuzo ya Nobel ya 2016 kwa maneno ya kiraia",
"David James Thouless\nDavid James Thouless (amezaliwa 21 Septemba, 1934) ni mwanafizikia kutoka nchi ya Uingereza. Hasa aligundua m . Mwaka wa 2016, pamoja na Frederick Duncan Michael Haldane na John Michael Kosterlitz, alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Alipewa tuzo kwa utafiti wake wa kinadharia katika maelezo ya tabia za mata katika hali karibu na sifuri halisi (ing. \"\"for theoretical discoveries of topological phase transitions and topological phases of matter\"\")\nProfesa John Chalker, mkuu wa idara ya Fizikia ya Kinadharia kwenye Chuo Kikuu cha Oxford anajaribu kueleza tuzo ya Nobel ya 2016 kwa maneno ya kiraia"
] | 29
|
Je, Togo ilipata uhuru mwaka upi?
|
[
"Togo\nMnamo Desemba 1956 wakazi wa Togo ya Kiingereza waliamua kwa kura kubaki na Ghana. Hivyo ni Togo ya Kifaransa pekee iliyopata uhuru mwaka 1960.",
"Historia ya Togo\nMnamo Desemba 1956 wakazi wa Togo ya Kiingereza waliamua kwa kura kubaki na Ghana. Hivyo ni Togo ya Kifaransa pekee iliyopata uhuru mwaka 1960.",
"Lome\nWakati wa uhuru mwaka 1960 Lome ikawa mji mkuu wa nchi huru ya Togo ikiwa na wakazi 80,000 walioongezeka kuwa 200,000 hadi 1970.",
"Historia ya Afrika\nVile vile, katika mwaka huohuo wa 1960 Congo (Kinshasa), Nigeria, Somalia, na Togo zikapata uhuru, na katika mwaka wa 1961 Sierra Leone na Tanganyika zikapata uhuru, na Afrika ya Kusini ikawa Jamhuri."
] |
[
"Historia ya Tanzania\nZanzibar ilipata uhuru wake tarehe 10 Desemba 1963. Uhuru wa usultani ukadumu muda mdogo tu. Mapinduzi ya tarehe 12 Januari 1964 yakamuondoa Sultani. Mauaji ya familia nyingi zenye asili ya Kiarabu yakafuata.",
"Seraphino Antao\nKenya ilipata uhuru mnamo Desemba 1963 na Seraphino alikuwa mwanariadha wa Kwanza kuipeperusha bendera ya Kenya katika Mashindano ya Olimpiki ya 1964 jijini Tokyo, Japan, lakini alikuwa mgonjwa na hakutia for a ilivyokuwa ikitarajiwa. . Alifika mkondo wa pili wa mita 200 kwa wanaume katika mashindano hayo lakini akatolewa katika awamu ya mjujo katika shindano la mita 100 ref>Sports and Elections Statistics: Men 100m Olympic Games 1964 Tokyo (JPN).",
"Togo ya Kijerumani\nTogo ilikuwa kielelezo cha koloni za Ujerumani hasa kwa sababu iliendelea vizuri kiuchumi. Kinyume cha koloni zote nyingine Togo haikupokea misaada kutoka Berlin lakini iliweza kugharamia utawala wake kutokana na mapato yake yenyewe.\nElimu ya shule ilibaki zaidi mkononi mwa misioni ya kikatoliki na kiprotestant. Mnamo mwaka 1910 nchi ilikuwa na shule 196 za kikatoliki na shule 163 za kiprotestant. Wakatoliki walikuwa pia na shule ya ufundi. Kwa ujumla Wamisionari Wajerumani walipendelea lugha za kienyeji kama lugha za mafundisho. Wamisionari wa Shirika la Misioni ya Bremen waliendesha shule zote kwa Kiewe.\nSerikali ya kikoloni ilikuwa na shule 4 pekee zilizofundisha kwa Kijerumani.",
"Togo ya Kiingereza\nMasharti ya UM yalikuwa nadharia tu kwa muda mrefu lakini yalipata umuhimu tena wakati wa uhuru. Kwa sababu hiyo wakazi wa maeneo ya Ghana yaliyowahi kuwa sehemu za eneo la Togo ya Kijerumani walipewa nafasi ya kuamua kama wangependelea kuendelea na Ghana au kuunganishwa tena na Togo yenyewe.",
"Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania\nKwa jumla kulikuwa na hali ya kutoridhika kati ya askari wa TR. Sababu yake ilikuwa matumaini ya kwamba uhuru ungeleta mabadiliko makubwa zaidi na nafasi za kupanda cheo baada ya kuondoka kwa maafisa wazungu. Lakini maafisa Waingereza waliendelea kuajiriwa na serikali ya Nyerere na tofauti kubwa katika mapato na hali ya makazi ya Wazungu na Waafrika ziliendelea. Hata kinyume askari waliowahi kuwa na mshahara wa juu kulingana na watumishi Waafrika wengine ya serikali waliona ya kwamba mapato yao hayakupanda ilhali mishahara kwa jumla iliongezeka zaidi. Zaidi ya hapo, serikali ya TANU ilituma vijana kutoka Umoja wa Vijana wa TANU kwa mafunzo ya kijeshi huko Israeli na baada ya kurudi walipewa ajira jeshini na wengine wao kupandishwa vyeo kupitia askari waliowahi kuhudumia miaka mingi.",
"Historia ya Rwanda\nTarehe 1 Julai 1962 Rwanda ilipata uhuru wake wa kisiasa. Wakati huu zaidi ya Watutsi 350,000 wameshakuwa wakikimbilia nchi jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizi za jirani walijaribu kushambulia utaratibu mpya. Iliyofuata ilikuwa uangamizaji wa kwanza wa Watutsi; zaidi ya 100,000 waliuawa na Wahutu. Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi iliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuita Watusi ndio \"Wadudu\". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbia Burundi, Uganda na Tanzania.",
"Togo ya Kijerumani\nWakati ule pwani la Togo ya leo ilikuwa bado eneo huru kati ya Pwani la Dhahabu (Ghana) chini ya Uingereza na eneo la Porto Novo (Benin) chini ya Ufaransa. Lakini Waingereza walisikitika ya kuwa biashara ya watu wa Aneho na Lome ilipanuka na nchi za Ulaya bila kuwaletea mapato ya ushuru kwa sababu bidhaa zilifika nje ya eneo lao."
] | 18
|
Muimbaji Celine Dion ana miaka mingapi?
|
[
"Céline Dion\nCéline Dion (amezaliwa tar. 30 Machi 1968) ni mwimbaji na mtunzi wa nyimbo mashuhuri za pop kutoka nchini Kanada. Alizaliwa katika mji wa Charlemagne mjini Quebec, Kanada. Yeye ni mdogo kuzaliwa katika familia ya watoto kumi na nne."
] |
[
"Céline Dion\nAlifikisha umri wa miaka 12, kaka yake alimpeleka kwa meneja wa urekodi aliyejulikana kwa jina la René Angélil, ambaye baadaye akaja kumwoa na kumzalia mtoto.\nKwa msaada wake, alifanikiwa kutoa albamu yake ya kwanza mnamo mwaka wa 1981, ambazo alikuwa akiimba kwa Kifaransa. Alitoa albamu yake ya kwanza kwa lugha ya Kiingereza kunako mwaka wa 1990.",
"The Best\nCeline Dion amewahi kuuimba wimbo huo live katika tamasha za muziki.",
"Let's Talk About Love\nLet's Talk About Love ni albamu ya mwimbaji Celine Dion iliyotolewa mnamo 18 Novemba 1997. Ni albamu yake ya tano inayotumia lugha ya Kiingereza, na ya 23 kwa jumla. \"Let's Talk About Love\" imeuza zaidi ya albamu milioni 31 kote duniani. Ndni yake, kuna wimbo wa \"My Heart Will Go On\" iliyoshinda tuzo ya \"Grammy Award\" na \"Academy Award\", na ilifika #1 kote duniani, na kuifanya iwe wimbo maarufu zaidi ya Celine Dion.",
"You're Still the One\n\"You're Still the One\" ulichaguliwa katika kategoria nne kwenye Grammy Awards mnamo 1999, huku ukishinda kategoria mbili tu. Ulishinda ukiwa kama Wimbo Bora wa Country na Mwimbaji Bora wa Kike wa Muziki wa Country na kupoteza Rekodi ya Mwaka na Wimbo wa Mwaka - badala yake Mkanada mwenzake , Celine Dion kachukua kwa ajili ya wimbo wake wa \"My Heart Will Go On\".",
"Baada ya Kristo\nLeo hii wataalamu wengi hukubaliana ya kwamba kasoro Ya Dionysio ni takriban miaka 4 - 8; yaani mwaka halisi wa kuzaliwa kwake Yesu ulikuwa kama miaka nne hadi nane kabla ya mwaka ambao tumezoea kuhesabu kama \"1\", kwa kuwa mwaka 4 K.K. ndipo alipokufa mfalme Herode Mkuu aliyejaribu kumuua akiwa mtoto mchanga.",
"A New Day ...\n\"A New Day ...\" ilikuwa aina ya sanaa za nyimbo zilizoimbwa na Céline Dion katika ukumbi wa viti 4000 iliyopo Caesars Palace mjini Las Vegas. Iliundwa na kuongozwa na Franco Dragone (anayojulikana kwa kazi yake kwa Cirque du Soleil na ikaanza tarehe 25 Machi 2003. \"A New Day ...\" ilianzisha mfumo mpya wa maonyesho ya burudani, kwa kuchanganya nyimbo, utendaji sanaa, ubunifu, na teknolojia. Ilichukua muda wa dakika 90. Dion alipewa mkataba wa miaka mitatu hapo awali, lakini kwa ajili ya mafanikio yake, yeye aliendelea kuimba kwa miaka miwili zaidi. \"A New Day ...\" ilimalizika 15 Desemba 2007, baada ya kuimbia kwa muda wa miaka 5 iliyo na zaidi ya maonyesho 700 na watazamaji milioni 3. Ilipata zaidi ya $400,000,000 kutoka maonyesho yote kwa jumla.",
"Kiboko (mnyama)\nKiboko huishi kwa miaka 40 mpaka 50. Kiboko aitwaye Donna, anayeishi akiwa na umri mkubwa kuliko wote sasa 57, huko Mesker Park Zoo katika Evansville, Indiana. Kiboko aliyewahi kuripotiwa kuwa na umri mkubwa zaidi aliitwa Tanga, aliishi huko Munich, Ujerumani na alifariki mnamo 1995 akiwa na umri wa miaka 61. Macho, masikio na pua za kiboko yapo juu ya fuvu la kichwa. Hii huwaruhusu kuzamisha sehemu kubwa ya mwili wao kwenye maji au matope na kupata ubaridi kujizuia na mwanga mkali wa jua. Mifupa yao imejengwa kuweza kubeba uzito wa mnyama wote. Kama mamalia wengine waishio majini, kiboko pia wana nywele chache za mwilini.",
"Angelina Jolie\nMnamo Tar. 15 Machi 2007, Jolie amemchukua mtoto mwingine wa kiume mwenye umri wa miaka mitatu, kutoka nchini Vietnam, wakamwita Pax Thien Jolie-Pitt, aliyezaliwa tarehe 29 Novemba 2003 na kutelekezwa katika hospitali za kienyeji, Ambako alipewa jina Pham Quang Sang.\nJolie alimchukua mtoto huyo kutoka kwenye kituo cha kulelea watoto yatima kiitwacho Tam Binh orphanage, cha mjini \"Ho Chi Minh City\".\nJina lake jipya ni mchanganyiko wa neno la kilatini \"Amani\" na la kivietnam \"Mawingu\" au Mbinguni\".",
"Beyoncé Knowles\nBeyoncé Giselle Knowles (alizaliwa 4 Septemba 1981), anayefahamika zaidi kwa jina moja Beyoncé ni mwimbaji wa R & B, mtunzi wa nyimbo, mtayarishaji wa rekodi, mwigizaji na mwanamitindo kutoka Marekani. Alizaliwa na kukulia Houston, Texas na alihudhuria shule mbalimbali zinazofunza sanaa. Pia alianza kushiriki katika mashindano ya kuimba na kucheza ngoma akiwa mtoto. Knowles alikuja kujulikana katika mwisho wa miaka ya 1990 kama mwimbaji kiongozi wa kikundi cha wasichana cha R & B, Destiny's Child. Kulingana na Sony, mauzo ya rekodi za Knowles, yakiunganishwa na yale ya kikundi cha Destiny's Child, yamezidi milioni 100."
] | 40
|
Lanhydrock House inapatikana wapi?
|
[
"Mto Fowey\nHuanzia kaskazini-magharibi ya Brown Willy katikae Bodmin Moor, hupitia Lanhydrock House, Restormel Castle na Lostwithiel,baadaye kunenepa katikiaMilltown kabla ya kujiunga na mtaro wa Uingereza katika Fowey. huvukika tu kwa kutumia vyombo vikubwa Kuna feri kati ya Fowey na Bodinnick. Barabara ya kwanza inyuvuka kwenda juu iko katika katika Lostwithiel. Mto huu una mito midogo saba, mkubwa ukiwa mto Lerryn. Sehemu ya Bonde la Fowey kati ya Doublebois na kituo cha reli Bodmin Parkway inajulikana kama bonde la Glynn (kutoka Glynn House, Cardinham). Bonde hili ni njia ya barabara kuu ya A38 na reli (iliyojengwa na kampuni ya Reli katika Cornwall mwaka wa 1859). Reli huwa juu ya ukuta wa mawe nane (tazama reli ya Cornwall )."
] |
[
"Kampuni ya Kittinger\nIdadi kubwa ya samani za Kittinger inapatikana katika sehemu ya West Wing katika jumba la White House huko Washington,DC.Wafanyikazi wa kupamba ndani ya nyumba wa Colonial Williamsburg Foundation walipewa kazi na Rais Richard Nixon ya kupamba ofisi za Rais. Kampuni ya Kittinger ndiyo iliyofanya kazi hii kwa sababu hii ndiyo kampuni pekee iliyoundia Colonial Williamsburg Foundation samani zao zinazofanana na zile za karne ya kumi na nane.. Katika muundo mpya wa ofisi zile,kuliongezwa meza ya mkutano na viti vya chumba cha mawaziri. Rais Nixon alilipa kwa hundi ya kibinafsi kulipia meza ile iliyoundwa na kampuni ya Kittinger na wakapatia White House. Kampuni inaendelea katika kazi ya utengenezaji huko Buffalo, NY.",
"Pembetatu ya Bermuda\nMeli kubwa ya milingoti mitano iliyojengwa katika 1919, \"Carroll A. Deering\" ilipatikana imeachwa kwenye ukingo mngumu wa bahari katika Diamond Shoals, karibu na Cape Hatteras, Carolina ya Kaskazini tarehe 31 Januari 1921. Fununu na zaidi za wakati huo zilionyesha \"Deering\" ilikuwa mwathiriwa wa uharamia, ulio na uwezekano wa kuhusiana na biashara haramu wakati wa Vikwazo, na uwezekano wa kushirikisha meli nyingine, SS \"Hewitt,\" ambayo ilitoweka wakati sawa na huo. Masaa machache tu baadaye, meli inayotumia mvuke isiyojulikana ilipita karibu na mwangaza wa meli kando ya njia ya \"Deering,\" na kupuuza ishara zote kutoka kwa mwangaza huu wa meli. Inakusudiwa kuwa huenda \"Hewitt\" ndiyo ilikuwa meli hii ya kilinge, na kuna uwezekano ilihusika katika kutoweka kwa mabaharia wa \"Deering\" .",
"Lincolnshire Echo\nKatika mwaka wa 2005, kiwanda cha uchapishaji cha Lincoln kilifungwa na uchapishaji kuhamishwa kutoka Grimsby na kisha kuhamishwa Derby. Huchapishwa mara kwa mara huko Stoke. Kutokana na hayo, gazeti hili huchapishwa mapema sana asubuhi na huwa tayari kuuzwa tangu saa 7 asubuhi. Hakuna uchapishaji wa toleo la pili na gazeti hili hutumia tovuti kutangaza habari mpya zilizotokea katika siku kucha. Jumba la Lincolnshire Echo liliuzwa Aprili 2009 kwa Chuo Kikuu cha Lincoln. \"Lincolnshire Echo\" lilihamisha ofisi zake hadi Witham Wharf, bado katikati mwa jiji.",
"Shule ya Upili ya Wavulana ya Starehe\nKiranja Mkuu wa na manaibu wake wawili mara nyingi inafahamika kama 'Red Lions'. Manaibu wawili ni sawa katika cheo. The House Viranja Wakuu kuchukua malipo ya bweni 12 ya nyumba na idara nyingine katika shule kama vile maktaba, michezo idara, Chapel na mkutano. Kila bweni huchukuliwa kuwa nyumbani kwa mwanafunzi katika miaka yake yote minne akiwa shuleni. Hapa, atakuwa akifanya urafiki na mwamana utakaomwelekeza na kumdumisha katika maisha yake yote Starehe. Mara nyingi, wanafunzi huelekea kujihusisha sana na mabweni yao hata baada ya kuondoka. Chini ya Vijanja wadogo, kuna wanafunzi wa kawaida au 'commoners' Viranja hutambulika vifuatavyo kulingana na madaraka yao:Kupanda kimadaraka kunaonyeshw akwa kutuzwa kwa nembo na pini zilizo hapo juu. Hizi huvaliwa upande wa kulia wa mkono wa koti .",
"Mauaji ya Halaiki ya My Lai\nSiku ile kikosi cha wanajeshi wa Marekani chini ya uongozi wa Luteni William Calley walipewa amri ya kutafuta wanamigambo ya Vietkong kijijini wakiambiwa ya kwamba Vietkong walijificha katika eneo lile. Waliambiwa ya kwamba wasingekuta watu raia mle lakini wategemee wanamigambo. Kikosi kilipoingia My Lai hawakuona wanamigambo bali wanawake, watoto na wazee watupu. Wakihofia ya kwamba Vietkong wanajificha kwenye vibanda na nyumba wanejeshi kadhaa walianza kufyatulia risasi kwenye nyumba na mauaji wa kwanza ya wanawake na watoto yalitokea kwa njia hiyo. Baada ya kusikia risasi watu walianza kukimbia kila upande na wanajeshi wengine walipiga risasi kwa wakimbiaji. Baada ya muda kidogo sehemu ya askari waliendelea kuwaua watu wote. Wakapitia nyumba kwa nyumba na kuua wajeruhiwa pia.",
"Hoteli ya Royal Palm (Miami)\nHoteli ilijengwa kwenye shamba la kijiji cha Tequesta. Mlima wa mchanga iliondolewa kufanyia njia ua la hoteli hiyo. Karibu fuvu 50 na 60 zilipatikana katika mlima huo na zikatupwa ndani ya mapipa. Baadhi ya fuvu hizo zilitolewa kama bidhaa za ukumbusho.\nHoteli hii ilikuwa kando ya Mto Miami kwa upande wa Kaskazini. Ua la hoteli liliizunguka hotel, takriban sudusi ya maili moja kwa urefu. Hoteli hii ilisemekana kuwa \"Ukoloni wa Kisasa\", yenye sifa ya \"pesa na mali\". Kulikuwa na vyumba 450 ya wageni. Chumba cha wastani cha wageni kilikuwa na kipimo cha futi 12 na futi 18, na 100 vilikuwa na bafu ya kibinafsi. Chumba kuu cha maakuli kiliweza kuwa na wageni 500. Chumba cha pili cha maakuli kilikuwa cha aya na watoto. Kulikuwa,pia, na vyumba vya maakuli vya kibinafsi. Kulikuwa na vyumba vya michezo,chumba cha kusikiza nyimbo na densi ,vyumba 100 vya kuvaa nguo na dimbwi la kuogelea. Chumba cha kuchamsha maji,chumba cha kuunda umeme,chumba cha kufulia nguo na chumba cha kuunda barafu vilikuwa katika jengo tofauti. Hoteli ilikuwa na wafanyikazi 300, miongoni mwao kukiwa na wapishi kumi na sita. Ingawa katika mji wa Miami kulikuwa na kifungu cha sheria, kilichosisitizwa na Julia Tuttle,kilichokataa uuzaji wa vinywaji vileo pahali popote mjini humo,Hoteli ya Royal Palm ilikuwa na kibali cha kuuza vinywaji hivyo katika miezi mitatu ya misimu ya utalii.1. Muir. P. 187",
"Rhino Charge\nRhino Charge ni tukio la kila mwaka, linalifanyika nchini Kenya, ambalo washindani wana kushindana kwenye njia mbaya wakitumia magari ya aina ya 4x4. Fedha zote zinazokusanywa hupewa chama cha Rhino Ark, ambacho husaidia kuhifadhi eneo la Aberdare. Washindani hutakiwa kulipa kiwango cha chini zaidi ya pesa za udhamini lakini kuna timu ambazo hupitisha kiwango hiki, rekodi iliyopo hadi sasa ni shilingi 9,393,552 na iliwekwa na timu ya gari nambari 5 ya Alan McKittrick, Bruce Knight, Charlie Hewitt-Stubbs, John Trundell, S. McKittrick, washindi wa tuzo lililodhaminiwa sana la David Schaeffer. Wadhamini wa muda mrefu kama Mike and Sarah Higgins wamekusanya shilingi 39,604,399 katika muda wa miaka 20.",
"Goat Island (New York)\nKisiwa kiliundwa kwa njia ya jiologia wakati wa mafungo ya karibuni ya maporomoko haya yalivyokata ndani ya kuta za Niagara. Mkondo wa mto Niagara umepasuka katika maporomoko mawili katika pade zake mbili. Katika 1959-60, upande wa mashariki wa kisiwa hiki ulipanuliwa karibu kwa ajili ya nyongeza yakiwanja cha kuegeza na helikopta. Jaza lilitokana na kuchimbwa kwa ajili ya ujenzi wa Robert Musa State Parkway. Upande wa magharibi wa kisiwa hiki unamalizwaa maporomoko haya polepole na hatimaye kisiwa chote kitaisha maporomoko yakiendelea kumaliza maeneo juu ya mto. Maji karibu kisiwa mbusi huwa na kina kifupi na kujaza miamba, Maeneo haya mara minigi huwa maeneo ya uokoaji au majaribio ya uokoaji.",
"Linah Kilimo\nKatika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2002 alichaguliwa kuwakilisha eneo bunge la Marakwet Mashariki kwa tiketi ya NARC. Wapinzani wake wa kisiasa walikuwa wamepinga kukimbilia kwake kwa kiti cha ubunge kwani msingi wao ulikuwa kwamba Linah hakuwa amepashwa tohara na hivyo basi hakuwa katika hali mwafaka ya kukimbilia ofisi ya umma.\nHata hivyo amefanya kazi kwa ufanisi pamoja na mashirika ya Kiserikali na yasiyo ya Kiserikali (NGO) huku lengo lao kuu likiwa kutokomeza ukeketaji. Pia amefanya kazi kwa ufanisi katika kuleta amani ya kudumu kati ya jamii ya Wapokot na jamii ya Wamarakwet. Jamii ya Wamarakwet na hasa wale wanaotoka katika eneo bunge ya Marakwet Mashariki walikuwa wamevamiwa na kuteswa vibaya sana na mashujaa wa Kipokot ambao walikuwa wezi wa kimabavu na ambao Serikali ya KANU ilikuwa imeshindwa kuwasimamisha licha ya kuwepo kwa Jeshi, Polisi na kijeshi cha polisi katika eneo hilo. Amani hii ilipatikana tu baada ya Serikali ya NARC kuchaguliwa mnamo Desemba mwaka wa 2002. Kama matokeo jamii hizi mbili sasa zinaishi kwa amani na utulivu.\nLina Kilimo pia amefanikiwa katika kuendeleza eneo bunge la Marakwet Mashariki, kwa kutoa ufadhili kwa shule za mitaa kwa njia ya vitabu, walimu zaidi, mipango ya chakula na hata nguo. Jebii amefanya kazi pamoja na Serikali kuboresha barabara ya kuingia katika eneo bunge hilo kupitia ujenzi wa barabara ya hali ya hewa zote (\"all-weather road\" kwa lugha ya kimombo) huku nia na lengo kuu likiwa kuweka lami katika barabara hiyo kwa muda usiyokuwa mrefu.\nKilimo Linah ameolewa kwa mhandisi anayehudumu katika Serikali na walijaliwa kuwa na wana watano."
] | 43
|
LL Cool J, alizaliwa mwaka gani?
|
[
"LL Cool J\nJames Todd Smith (amezaliwa tar. 14 Januari 1968) ni rapa na mwigizaji wa filamu kutoka nchini Marekani. Anafahamika zaidi kwa jina la kisanii kama LL Cool J. LL Cool J inasimama kwa \"Ladies Love Cool James\". Anajulikana sana kwa maballad yake ya kimahaba kama vile \"I Need Love\", \"Around the Way Girl\" na Hey Lover\", vilevile kuanzisha kuanzisha hip-hop kama vile \"I Can't Live Without My Radio\", \"I'm Bad\", \"The Boomin' System\", na \"Mama Said Knock You Out\". Pia amepata kuonekana katika filamu kadha wa kadha. LL Cool J ni mmoja kati ya wasanii wachache wa hip hop wa zama zake kuweza kupata mafanikio makubwa katika zake za kurekodi kwa zaidi ya makumi mawili. Ametoa takriban albamu kumi na mbili na kompilesheni ya vibao vikali kadhaa mpaka sasa, na albamu yake ya mpya kuwa ya mwaka wa 2008,s \"Exit 13\", ambayo ni ya mwisho kwa LL kufanya kazi na Def Jam Recordings. Kwa sasa anaishi mjini Manhasset, New York na watoto wake wa nne na mke wake."
] |
[
"Rock the Bells\nRock the Bells ni single ya tatu kutoka katika albamu ya kwanza ya LL Cool J, Radio. Ilitolewa mnamo mwaka wa 1985 na Def Jam Recordings. Ilitungwa na LL Cool J na kutayarishwa na Rick Rubin. Rock the Bells ilifikia kiwango cha #17 kwenye chati za Hot R&B/Hip-Hop Songs. Wimbo huu baadaye ukaja-kusampuliwa na yeye mwenye LL Cool J kwa ajili ya wimbo wake wa \"Mama Said Knock You Out\", kutoka katika albamu yake ya yenye jina sawa na la wimbo huo.\nEminem, DJ Jazzy Jeff na The Roots waliuimba wimbo huu wa “Rock The Bells” kwenye VH1 Hip Hop Honors ikiwa kama kuonyesha shukrani kwa Def Jam.",
"You'll Rock\nYou'll Rock ni single ya tano kutoka katika albamu ya kwanza ya LL Cool J, You'll Rock. Ilitolewa mnamo mwaka wa 1985 katika studio ya Def Jam Recordings na ilitungwa na kutayarishwa na Rick Rubin na LL Cool J. Wimbo ulihahakiwa kuwa kwamba ndiyo wa nne katika single zote kutoka albamu na wa mwisho kupata mafanikio katika orodha hiyo, kwa kushika kilele cha #59 kwenye chati za Hot R&B/Hip-Hop Songs.",
"10 (albamu)\n10 ni jina la kutaja albamu ya tisa ya rapa wa Kimarekani, LL Cool J. Albamu ilitolewa mnamo tar. 15 Oktoba, 2002 na studio za Def Jam Recordings. Albamu iliweza kushika chati nafasi ya pili katika chati za \"Billboard\" 200 huko nchini Marekani. LL Cool J na \"10\" amefikisha lengo la Def Jam katika historia, kwa kuwa msanii msanii wa kwanza kuwa na albamu kumi kwenye Def Jam (mbali na mpango mzima wa albamu kumi na tatu) akiwa chini ya studio moja.\nAlbamu – \"Billboard\" (Amerika ya Kaskazini)\nSingle – \"Billboard\" (Amerika ya Kaskazini)",
"I'm Bad\n\"I'm Bad\" (pia huandikwa I'm BAD) ni single ya kwanza kutoka katika albamu ya pili ya LL Cool J, \"Bigger and Deffer\". Ilitolewa mnamo mwaka wa 1987 kupitia studio za Def Jam Recordings na ilitayarishwa na kundi la watayarishaji The L.A. Posse na LL Cool J mwenyewe, na Russell Simmons akiwa kama mtayarishaji mkuu wa single. I'm Bad imefanya chati kadhaa katika \"Billboard Charts\", ikiwa pamoja na 84 kwenye Billboard Hot 100, 4 kwenye Hot R&B/Hip-Hop Songs, 23 kwenye Hot Dance Music/Maxi-Singles Sales, 34 kwenye Hot Dance Music/Club Play na 7 kwenye UK Singles Chart. Single hii ilifuatiwa na \"I Need Love\" na \"Go Cut Creator Go\".",
"I Can't Live Without My Radio\n\"I Can't Live Without My Radio\" ni single kiongozi kutoka katika albamu ya kwanza ya LL Cool J, \"Radio\". Ilitolewa mnamo mwaka wa 1985 kupitia studio za Def Jam Recordings na zote -litungwa na kutayarishwa na LL Cool J na Rick Rubin. Wimbo huu ulipata mafanikio mwanana, imeiweka katika nafasi ya #15 kwenye chati za Hot R&B/Hip-Hop Singles & Tracks na mpaka leo hii huhesabiwa na wengi kwamba ni moja kati ya nyimbo bora za hip hop zilizowahi kurekodiwa. \"I Can't Live Without My Radio\" ilitolewa na single -liofuatia I Can Give You More.",
"I Need a Beat\nI Need a Beat ni single ya kwanza kutoka kwa rapa, LL Cool J, na ni moja kati ya matoleo mawili ya Def Jam Recordings kuwa na nembo katalogi ya namba, sambamba kabisa na Beastie Boys' \"Rock Hard\". Ilitolewa mnamo mwaka wa 1984 kwa ajili ya Def Jam Recordings, imetayarishwa na Rick Rubin na kutungwa na Rubin, LL Cool J na Adam Horovitz wa Beastie Boys. Baadaye wimbo ulirudiwa tena na kutumbukizwa kwenye albamu yake ya kwanza ya \"Radio\".",
"Mr. Smith\nMr. Smith ni jina la kutaja albamu ya sita ya rapa LL Cool J. Albamu ilitolewa mnamo mwaka wa 1995. Baada ya kutofanya vizuri katika albamu iliyopita ya \"14 Shots to the Dome\", lakini hapa imekuwa kama msanii aliorudi kundini, kwa kuweza kwenda kwenye Platinum 2x na kuingiza vibao vikali vitatu kwenye 10 bora, \"Hey Lover\", \"Doin' It\", na \"Loungin\". Albamu hii ipo tofauti kabisa na matoleo yake ya awali, ambayo yenyewe yamefokasi sana katika hardcore rap, katika albamu hii LL anaonekana kuzingatia zaidi kwenye maballad ambayo hadi sasa anatamba nayo. Albamu hii ilikuwa ya kwanza katika albamu zake kuwa na ujumbe wa Parental Advisory.",
"I Can Give You More\nI Can Give You More ni single ya pili kutoka katika albamu ya kwanza ya LL Cool J, Radio. Ilitolewa mnamo mwaka wa 1985 chini ya studio ya Def Jam Recordings na ulitungwa na kutayarishwa na Rick Rubin na LL Cool J. Wimbo ulishika nafasi ya #21 kwenye chati za Hot R&B/Hip-Hop Songs. I Can Give You More lilikuwa toleo jengine la single ya I Can't Live Without My Radio upande-B.",
"All World: Greatest Hits\nAll World: The Greatest Hits ni albamu ya kwanza ya vibao vikali vya kompilesheni kutoka kwa msanii wa hip hop, LL Cool J, ambayo imetolewa mnamo mwaka wa 1996. Inachukua nafasi kutoka kazi zake za awali za Def Jam, \"Radio\", mpaka albamu yake ya mwaka wa 1995 \"Mr. Smith\". All World imetunukiwa platinum na RIAA."
] | 29
|
Je,Kampuni ya Kenya Breweries Limited ilianza mwaka upi?
|
[
"Bia\nViwanda vya bia vilianza kufanya biashara katika mji wa Dar es Salaam mwaka 1906 wakati wa ukoloni wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Bwana Wilhelm Schultz alikuwa mmilikaji wa biashara hii. Biashara hii iliharibiwa na Waingereza katika mwaka 1916, lakini biashara ingine ilianza kuuza bia katika mwaka wa elfu moja mia tisa ishirini na mbili nchini Kenya na Tanzania. Biashara hii mpya iliitwa “Kenya Breweries Limited.”",
"East African Breweries\nKenya Breweries ilianzishwa mwaka wa 1922 na walowezi wawili, George na Charles Hurst. Kufikia mwaka wa 1990, wengi wa wanahisa walikuwa kwenye kampuni hii walikuwa Wakenya na ilikuwa na mafanikio sana."
] |
[
"East African Breweries\nTanzania Breweries ilikuwa imeanzishwa na Kenya Breweries katika miaka ya 1930. Baada ya kutaifishwa mwaka wa 1967, Tanzania Breweries ilikumbwa na usimamizi mbaya . Hata hivyo, mwaka wa 1993 serikali ya Tanzania aliingia mkataba na South African Breweries Limited kuendesha shughuli za Tanzania Breweries. South African Breweries ni mojawapo wa makampuni makubwa ya kutengeneza pombe na yenye ufanisi mkubwa duniani. Waliimarisha Tanzania Breweries kwa kasi ya ajabu, huku uzalishaji ukiongezeka kwa karibu mara tatu kwa kipindi cha miaka mitatu.",
"East African Breweries\nMwaka wa 2002 East African Breweries Limited (EABL) na SABMiller Plc. walikubaliana kubadilishana hisa zao kwenye kumpuni walizomiliki: Kenya Breweries Limited na Tanzania Breweries Limited. EABL ilipewa 20% ya hisa za Tanzania Breweries. SABMiller Plc. nayo ilipewa 20% ya umiliki kwenye Kenya Breweries. Mnamo mwaka wa 2003, Kenya Breweries ilitumia karibu 6% ya maji ya Nairobi.",
"Njenga Karume\nBaadaye aliendesha kampuni ya Nararashi Distributors, ambayo walikuwa na wadhifa wa kusambaza bidhaa za Kenya Breweries Limited (KBL). Baadaye Castle Brewing Kenya Limited, kampuni ndogo(subsidiary) nchini Kenya ambacho kampuni yake kuu ni South African Breweries (SAB) iliundwa, huku Karume akiteuliwa kama mkurugenzi wake. Karume mwenyewe alitaka kusambaza bidhaa za kampuni zote mbili, lakini KBL iliofia ushindani na kuamua kufutilia mbali mkataba wa Karume wa usambazaji ili kudhuru biashara yake. Karume alichukua kesi mahakamani na kusema kuwa kufutilia mbali kwa mkataba wake haukuwa na ushahidi. Mahakama Kuu kwanza iliamuru KBL kumlipa Karume Shilingi za Kenya 231 kwa uharibifu lakini kutokana na rufaa uamuzi ulipinduliwa na Karume aliambiwa kulipa KBL kwa mashtaka. Kutokana na malipo hayo kwa KBL, Karume aliathiriwa na uhaba wa fedha. Aliendelea kusambaza bia ya Castle kwa muda hadi SAB ilipoondoka Kenya, hatimaye kukamilisha biashara yake ya usafiri.",
"Tusker (pombe)\nTanzania Breweries ilianzwa na Kenya Breweries katika miaka ya 1930. Baada ya kugeuzwa kuwa ya taifa mwaka wa 1967, Usimamizi wa Tanzania Breweries ulihofia. Hata hivyo, mwaka wa 1993 serikali ya Tanzania ilishirikiana na South African Breweries Limited katika uendelezaji wa Tanzania Breweries. South African Breweries ni moja ya makampuni kubwa ya utengenezaji wa pombe katika dunia. Iliweza kugeuza Tanzania Breweries kwa kasi ,kwa kuongeza utengenezaji karibu mara tatu katika muda wa miaka mitatu.",
"Tusker (pombe)\nMwaka wa 2002 East African Breweries Limited (EABL) na SABMiller plc. zilibadilishana faida ya hisa: Kenya Breweries Limited na Tanzania Breweries Limited. EABL ilipokea asilimia 20% ya mali ya Tanzania Breweries. SABMiller plc. ilipokea asilimia 20% ya mali ya Kenya Breweries. Mwaka wa 2003, Kenya Breweries ilitumia karibu asilimia 6% ya maji ya Nairobi.",
"East African Breweries\n\"Tusker\" ndio brandi kuu ya East African Breweries na zaidi ya 30% ya soko la Kenya la bia huuza zaidi ya hektolita 700,000 kila mwaka. Tusker pia ndio brandi ya bia kuu katika kundi la makampuni la Diageo . Ina kiwango cha pombe cha 4.2% abv . Brandi hii ilianzwa kuuzwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 1923, muda mfupi baada ya mwanzilishi wa Kenya Breweries Ltd, George Hurst, aliuawa na ndovu kwenye ajali ya uwindaji. Ilikuwa mwaka huu ambapo alama ya ndovu, inayotambulisha Tusker Lager, ilikubalika. Kaulimbiu \"Bia Yangu, Nchi Yangu\", maana yake \"My Beer, My Country\" katika Kiswahili.",
"Bia\nMwanzoni waafrika wa mashariki hawakuruhusiwa kununua bia katika chupa. Bali kanuni ilibadilishwa baada ya sheria mpya ilipopitishwa mwaka wa 1947. “Kenya Breweries Limited” au “KBL” na “East African Breweries Limited” au “EABL” zilitawala soko la bia kwa muda mrefu kabisa.",
"Katiba ya Kenya\nKatiba ya mwaka 1963, ilirekebishwa katika mwaka 1969. Marekebisho yalibadilisha Kenya kutoka mfumo wa shirikisho, uliokuwa ukijulikana kama mfumo wa majimbo, hadi mfumo wa umoja na kuifanya bunge iwe ya chumba kimoja. Serikali ilibadilika kutoka mfumo wa kibunge hadi mfumo wastani wa kirais, ikiwa na rais mwenye nguvu zaidi. Ulinzi wa orodha ya haki ulipunguzwa. Marekebisho mengine yalifanyika mwaka 1982. Yaliifanya Kenya kuwa nchi ya chama kimoja.",
"Tusker (pombe)\n\"Tusker\" ndiyo bidhaa kuu ya East African Breweries iliyo na zaidi ya asilimia 30% ya soko Kenya ya bia ikiuzwa zaidi ya hektolita 700.000 kwa mwaka. Tusker ndiyo bia kubwa katika kundi la makampuni Diageo .. Iliuzwa mara ya kwanza katika mwaka wa 1923, muda mfupi baada ya mwanzilishi wa Kenya Breweries Ltd, George Hurst, aliuawa na tembo wakati wa ajali uwindaji . Ilikuwa mwaka huu kwamba alama ya tembo , iliwekwa katika chupa ya pombe ya Tusker Lager. Msemo \"bia Yangu, Nchi Yangu\", maana yake \"My Beer, My Country\" katika kimombo."
] | 32
|
Je,Samir Nasri alizaliwa lini?
|
[
"Samir Nasri\nSamir Nasri (amezaliwa 26 Juni 1987) ni mchezaji wa kandanda wa kimataifa wa Ufaransa ambaye anaichezea klabu ya Arsenal katika ligi kuu ya Uingereza."
] |
[
"Samir Nasri\nNasri amekuwa akihusika katika timu ya taifa ya Ufaransa kwa muda mrefu, kuanzia timu za vijana wenye umri wa miaka 16, 17, 18, 19 na 21. Alikuwa katika timu ambayo ilishinda mashindano ya UEFA ya vijana wasiozidi umri wa 17 mwaka wa 2004, na alifunga bao la ushindi katika mechi ya mwisho. Nasri alicheza mechi yake ya kwanza ya timu kuu mnamo 28 Machi 2007 dhidi ya Austria, katika mechi ya kirafiki ya nyumbani akiwa na umri wa miaka 19. Alitoa pasi ndani ya boksi ambayo mchezaji mwenzake, Karim Benzema,alifunga bao la kipekee la mechi. Alifunga bao lake la kwanza katika mechi yake ya tatu katika timu kuu na Ufaransa ilishinda mechi hiyo, ambayo pia ilikuwa mechi ya kufuzu kushiriki katika kombe la Euro 2008,1-0 dhidi ya Georgia tarehe 6 Juni 2007. Nasri alitajwa katika kikosi cha mwisho cha Euro 2008 cha Raymond Domenech akiwa na umri wa miaka 20; alikuwa mmoja wa wachezaji wenye umri mdogo katika kikosi cha Kifaransa kuteuliwa katika mashindano ya Euro 2008. Alicheza mechi mbili kama mbadala na kucheza dakika 32.",
"Samir Nasri\nNasri alianza kuicheza Marseille akiwa na umri wa miaka 9. Alianza kucheza katika Ligue 1 (ligi kuu ya Ufaransa) katika msimu wa 2004/2005 akiwa na umri wa miaka 17, na alianza mechi 13 na akaja kama mbadala mechi 11, na kufunga bao moja. Msimu uliyofuata ulimpa uzoefu katika kombe la UEFA (mechi 10 bila kufunga bao) na kombe la Intertoto (alicheza mechi moja na kujunga bao moja). Katika msimu wa 2006/2007 alifunga bao lake la kwanza la mwaka katika Ligue 1 msimu ukielekea kuisha tarehe 29 Aprili 2007, wakati alianza mechi dhidi ya FC Sochaux-Montbéliard na alisaidia timu yake kushinda 4-2. Ushindi huu uliifanya Marseille kupanda hadi nafasi ya nne katika Ligi 1 mechi nne zikisalia, na hivyo basi kuiweka Mairseille katika nafasi ya kufuzu katika Kombe la UEFA. Nasri alikuwa katika kikosi kilichoshindwa katika fainali ya Coupe de France mwaka 2006 dhidi ya Paris Saint-Germain na pia alikuwa katika kikosi kilichoshindwa katika fainali dhidi Sochaux mwaka wa 2007.",
"Samir Nasri\nWazazi wa Nasri walihamia Ufaransa kutoka Algeria. Babake anatoka Constantine na mama yake ni raia wa Biskra. Alilelewa katika sehemu ya La Gavotte Peyret,kitongoji kilicho kaskazini mwa Marseille. Mara nyingi yeye alicheza mitaani, ambapo alijifunza ujuzi wake. Alikuwa anaichezea timu ya genge ya mtaa, lakini baada ya vurugu nyingi, wazazi wake walimsaini katika klabu ya Pennes Mirabeau akiwa na umri wa miaka sita. Nasri mwenyewe amedai kuwa malezi yake ngumu imemsaidia katika jitihada zake za kucheza kandanda ya Utaalamu, \"kama ninaweza kuwa na ujasiri wa kutosha wa kuonana ana kwa ana na kisu, nina ujasiri wa kutosha nina ujasiri wa kutosha kupambana mkabiliano mgumu. Aliichezea timu ya Pennes kwa muda wa misimu miwili kabla ya kutazamwa na Olympique de Marseille mwaka wa 1996.",
"Samir Nasri\nNasri amelinganishwa na mchezaji wa kitambo wa Arsenal, Robert Pires, na Arsène Wenger ambaye pia amemweleza Nasri kama mchezaji mwenya kasi na mchezaji maalam anayeweza kucheza katika sehemu tofauti uwanjani na pia kuwaona wachezaji wenzake uwanjani.",
"Samir Nasri\nNasri alifunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya West Bromwich Albion, baada ya dakika nne ya mechi ya kwanza ya msimu, tarehe 16 Agosti 2008. Tarehe 27 Agosti katika mechi ya pili ya raundi ya kufuzu katika kombe la mabingwa barani Ulaya, Nasri alifunga bao katika dakika ya 26 dhidi ta FC Twente. Tarehe 8 Novemba 2008, Nasri alifunga mabao yote mawili ya Arsenal' katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Manchester United. Tarehe 21 Machi, Nasri alifunga bao tena Arsenal ilipoishinda Newcastle 3-1 katika uwanja wa St James 'Park. Alitamatisha msimu wake wa kwanza na Arsenal na mabao 7 na usaidizi 5.",
"Samir Nasri\nTarehe 20 Mei 2007, Nasri alitajwa kama mchezaji mchanga bora wa mwaka katika Ligue 1 mbele ya Jimmy Briand na Karim Benzema. Alitajwa pia kama mchezaji bora wa mwaka wa Marseille baada ya kupata asilimia 62 ya kura kutoka kwa mashabiki. Aidha, kama wachezaji wachanga wengine, alitajwa kama \" zizou mpya \" kutokana na ujuzi wake wa kuchenga na mtazamo.",
"Samir Nasri\nHapo awali alikuwa mchezaji wa kawaida wa timu ya Ufaransa katika kiwango cha vijana. Nasri alitajwa katika kikosi cha Euro mwaka wa 2008 lakini hakupata muda mwingi wa kucheza. Tangu wakati huo, amejiimarisha kama mchezaji wa kawaida katika timu ya taifa.",
"Samir Nasri\nYeye hutumia mguu wa kulia sanasana kucheza, na kwa ujumla hucheza kama mshambulizi mpana katika klabu yake ya Arsenal, lakini pia ametumika katika kiungo kati kwa majukumu ya kushambulia na kulinda wakati amehitajika. Amesifiwa na wengi kama \" zizou mpya \" (yaani mchezaji matata wa kitambo wa ufaransa, Zinedine Zidane) baada ya kufurahisha katika klabu ya Marseille wakati wa ujana wake.",
"Isa\nNabii Isa aliletwa kwa wanadamu kufikisha ujumbe kwao wa kuwafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja, hana mwenzake, na kuwa Yeye pekee ndiye mwenye kustahili kuabudiwa kwa haki. Ujumbe huu ndio ujumbe uleule uliotumwa kwa Mitume na Manabii wote kwa wanadamu ili kuwaongoza, naye alikuja kutilia mkazo na kusisitiza jambo hili na kuzipa nguvu tume za Mitume na Manabii waliopita."
] | 29
|
Je,Alain Didier Zokora Deguy alizaliwa lini?
|
[
"Didier Zokora\nAlain Didier Zokora Deguy (amezaliwa 14 Desemba 1980 katika mji mkuu wa Abidjan) ni mchezaji wa mpira wa miguu kutoka nchini Cote d'Ivoire (Ivory Coast), ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya huko Hispania, maarufu ya Sevilla FC na pia timu ya taifa ya Cote d'Ivoire."
] |
[
"Didier Zokora\nZokora nikiungo muhimu katika klabu yake na timu yake ya taifa ya Cote d'Ivoire,yeye ni mchezaji mzuri wa katikati ambae anatumia ufundi wa hali ya juu katika uchezaji wake na amezungumziwa na wafatilia mpira wa miguu wengi kua ni mchezaji ambae anatumia akili na mbinu katika uchezaji wake.",
"Didier Zokora\nZokora alianza kuichezea timu yake ya taifa ya [[Cote d'Ivoire]] mwaka 2000 lakini bila kua kiungo muhimu kutokana na umri wake mdogo nakuchezea katika ligi ya nyumbani kwani timu ya taifa ya [[Cote d'Ivoire]] hutegemea zaidi wachezaji wanaocheza nje, alipotoka nakujiunga na klabu ya huko Ubelgiji ndio alianza kucheza vizuri katika timu ya taifa nakushiriki katika mechi nyingi kama kiungo muhimu lakini alidhihirika zaidi nakupata umashuhuri zaidi mwaka 2005 katika mashindano yakugombea tiketi yakuelekea katika kombe la dunia lililofanyika huko [[Ujerumani]] waliweza kunyakua tiketi kutoka katika mikono ya timu kali kama [[Misri]] na [[Kameruni]] na huo mwaka waliweza kuifunga [[Misri]] nyumbani [[Misri]] 2-1 na huko [[Cote d'Ivoire]] 2-0 timu [[Cote d'Ivoire]] huo mwaka ilionekana timu kali sana ambayo ni vigumu kufungwa kiuraisi ilishiriki katika [[kombe la Mataifa ya Afrika]] misri ilitoa timu nyingi kama [[Nigeria]] na [[Kameruni]], walifika fainali lakini walifungwa kwa mapenelti na waandalizi wa kombe hilo [[Misri]].[[Jamii:Waliozaliwa 1980]]\n[[Jamii:Wachezaji mpira wa Cote d'Ivoire]]\n[[Jamii:Watu walio hai]]",
"Didier Zokora\nZokora alianza kucheza mpira katika katika ujana wake katika klabu ya ASEC Mimosas(Cote d'Ivoire) mwaka 1999/2000,huo mwaka alionekana ni miongoni mwa wachezaji wazuri katika klabu yake hiyo ya ASEC,basi baadhi ya klabu za Ulaya zilipendelea kumnunua,katika mwaka 2000 klabu ya Ubelgiji ya KRC Genk iliweza kupata fursa yakumnunua,Zokora alicheza katika klabu hiyo hadi mwaka 2004 na aliichezea klabu hiyo katika mechi 126 na alifunga goli li moja tu,nakuanzia mwaka 2004 alijiunga na klabu mashuhuri ufaransa ya Saint-Étienne huko ndipo alianza kuonekana kua nyota au kua mashuhuri katika ulimwengu wa mpira maana uchezaji wake katika timu hiyo ya Ufaransa ulikua mzuri sana na katika timu yake ya taifa maana alisaidia timu yake kushika nafasi za mwanzo katika Ligue 1(Ligi ya kwanza) ya Ufaransa na alichezea klabu hiyo ya ufaransa mechi 66 na alifunga magoli mawili tu,Uchezaji wake mzuri ulipeleka klabu nyingi kubwa kubwa barani Ulaya kupendelea kumnunua lakini klabu ya Uingereza iliweza kumnunua kwani ilitoa pesa nyingi na ilikua mwaka 2006 na aliichezea klabu hiyo ya[[Uingereza kuanzia mwaka 2006 hadi mwaka 2009.",
"Zola D\nDavid Michael Mlope au Zola D (amezaliwa tarehe 21 Januari 1980) ni mwimbaji wa muziki wa hip hop laini kutoka nchini Tanzania. Huenda akawa anafahamika zaidi kwa vibao vyake kadhaa vilivyoweza kutikisa jiji la Dar es Salaam kwa kipindi kirefu; vibao hivyo ni: \"Jana sio Leo\" na \"Moto wa Tippa\".",
"DJ Yella\nDJ Yella ni jina la kisanii la Antoine Carraby (amezaliwa tar. 11 Desemba 1967) ni DJ, mtayarishaji wa mzuiki na mwongozaji wa filamu kutoka mjini Compton, California, Marekani. Yella pia alikuwa mmoja wa wanachama wa kundi la muziki linalojulikana kama World Class Wreckin' Cru akiwa pamoja na Bw. Dr. Dre. Baadaye akaja kuwa mmoja wa waanzilishi wa kundi la muziki wa hip hop maarufu kama N.W.A. (akiwemo Yella, Dre, Ice Cube, MC Ren, na Eazy-E). Akiwa pamoja na Dre Yella akafanikisha kurekodiwa kwa albamu ya mwenziwao (Eazy-E). Albamu ilikwenda kwa jina la \"Eazy Duz It\".",
"Juliana Daniel Shonza\nJuliana Shonza alizaliwa tarehe 23 Aprili 1987 katika mkoa wa Mbeya. Mwaka 1995 alianza elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Sinde. Alihitimu elimu yake ya sekondari katika shule ya Kibasila mwaka 2005 na baadaye kuhitimu kidato cha sita shule ya sekondari Dakawa mwaka 2008.\nMwaka 2008 alifanya Shahada yake ya kwanza ya Sayansi ya Jamii katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadaye aliendelea na masomo ya Shahada ya pili katika fani hiyo mwaka 2013 kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma.",
"Raymond Aaron\nRaymond-Claude-Ferdinand Aron (14 Machi 1905 – 17 Oktoba 1983) alikuwa ni mwanafalsafa kutoka nchini Ufaransa, Mwanasosholojia, Mwandishi wa habari na mtaalamu wa masuala ya siasa.\nAnafahamika pia kutokana na uhusiano wake wa muda mrefu wa kirafiki na wakati mwingine wa kiuhasama na Jean-Paul Sartre. . Pia anafahamika zaidi kutokana na kitabu chake kilichotoka mwaka 1995, kilichofahamika kwa jina la \"The Opium of the Intellectuals\".\nAron pia aliandika kwa undani kuhusu mada nyingine nyingi katika sosholojia, habari na filosofia. Akizungumzia kuhusu undani na ubora wa kazi za Aron, mwandishi na mwanahistoria James R. Garlan ameandika kuwa, ijapokuwa anaweza kufahamika zaidi nchini Marekani, lakini Raymond Aron, anatajwa kuwa ni mtu maarufu sana miongoni wa wasomi wa nchini Ufaransa wa karne ya ishirini.",
"Nelly Sachs\nNelly Leonie Sachs (10 Desemba 1891 – 12 Mei 1970) alikuwa mwandishi na mshairi Myahudi kutoka nchi ya Ujerumani. Mwaka wa 1940 alisaidiwa na rafiki yake Selma Lagerlof kukimbia ukatili wa WaNazi na kuhamia Sweden. Katika mashairi na tamthiliya zake alieleza mateso ya Wayahudi, k.m. katika tamthiliya \"Eli: Juu ya Mateso ya Israel\" (kwa Kijerumani \"Eli: Ein Mysterienspiel vom Leiden Israels\") iliyotolewa mwaka wa 1951. Mwaka wa 1966, pamoja na Shmuel Yosef Agnon alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.",
"Didier Zokora\nMwaka [[2009]] tar 8 [[Julai]], klabu ya Tottenham ilikubali kumuuzisha mchezaji wake huyo muhimu kwenye klabu ya [[Sevilla]] ya [[Uhispania]] kiwango cha pesa hakikutangazwa,klabu hiyo inashiriki katika Ligi ya kwanza ya [[Uhispania]]"
] | 45
|
Bahari ya Atlantiki iko na ukubwa wa kiasi gani?
|
[
"Atlantiki\nAtlantiki ni bahari kubwa inayotenganisha Amerika upande wa magharibi na Afrika na Ulaya upande wa mashariki. Eneo lake ni kilometa za mraba 106,200,000 au sehemu ya tano ya uso wa dunia pamoja na bahari za pembeni kama bahari ya Baltiki na Mediteranea. Hivyo ni bahari kubwa ya pili duniani baada ya Pasifiki. Bila bahari hizi za pembeni eneo lake ni kilometa za mraba 82,400,000."
] |
[
"Atlantiki\nFunguvisiwa muhimu ni: \nvisiwa vya Faroe, visiwa vya *Azori, visiwa vya Madeira, visiwa vya Kanari, visiwa vya Cabo Verde, visiwa vya Karibi (pamoja na Kuba), visiwa vya Britania (pamoja na Uingereza na Ueire - Ireland, visiwa vya *Bermudas na vingine.\nMikondo ya Atlantiki inatawala hali ya hewa katika nchi zinazoongozana bahari. Kati ya mikondo hizi ni mkondo wa ghuba la Mexiko kutoka eneo la visiwa vya Karibi ukivuka Atlantiki na kubeba maji ya moto (ambayo bado ni vuguvugu kiasi wakati wa baridi) hadi pwani la Ulaya. Mkondo huu umesababisha ya kwamba sehemu kubwa ya Ulaya ina hali ya hewa ya wastani bila joto au baridi kali mno na mvua nyingi hivyo kuhakikisha rutuba ya bara. Bandari za Ulaya hubaki bila barafu hadi kaskazini kabisa.",
"Mgongo kati wa Atlantiki\nVilele vya juu vya milima hii inaonekana juu ya UB kama visiwa. Safu hii ya milima imetokea mahali ambako mabamba ya gandunia yanaachana: bamba la Ulaya-Asia na bamba la Amerika ya Kaskazini katika Atlantiki ya Kaskazini, halafu bamba la Amerika ya Kusini na bamba la Afrika katika Atlantiki ya Kusini.",
"Bahari ya Aktiki\nBahari ya Aktiki iko kati ya pwani za Asia ya Kaskazini, Alaska na Kanada katika Amerika ya Kaskazini, Greenland na Skandinavia (Ulaya). Eneo lake ni 14.056 km². Kati ya Greenland na Skandinavia kuna uwazi kubwa unaojifungua kwa Atlantiki ya Kaskazini na mlango wa Bering unaunganisha bahari hii na Pasifiki.",
"Mgongo kati wa Atlantiki\nKutambuliwa kwa safu hii kuliweka msingi kwa nadharia ya upanuzi wa misingi ya bahari unaosababisha mwendo wa mabamba ya gandunia.\nVisiwa ambavyo ni vilele vya milima ya mgongo huu ni kama vifuatavyo (katika mabano ni majina ya vilele vya juu na kimo):\nNusudunia ya kaskazini (Atlantiki ya Kaskazini):",
"Atlantiki\nBeseni yake ina umbo kama \"S\". Kina ya wastani ni mita 3,332; kina kikubwa katika mfereji wa Puerto Rico kinafikia mita 8,605. Upana wa bahari ni kati ya km 2,648 kati ya Brazil na Liberia hadi km 4,830 kati ya Marekani na Afrika ya Kaskazini.",
"Mgongo kati wa Atlantiki\nMgongo kati wa Atlantiki ni safu ya milima chini ya maji ya bahari ya Atlantiki inayoelekea kutoka 87°N (333 km kusini kwa Ncha ya kaskazini) hadi kisiwa cha Bouvet kusini mwa dunia kwenye 54°S.",
"Jiografia ya Urusi\nSehemu kubwa ya mipaka ya nje iko kwenye maji. Pwani ndefu ni pwani ya kaskazini iliyopo ng'ambo ya Mzingo Aktiki; kwa hiyo pwani hiyo inafunikwa na barafu ya bahari kwa sehemu kubwa ya mwaka isipokuwa bandari ya Murmansk inayopokea maji fufutende kiasi kutoka mkondo wa ghuba. Bahari Aktiki, Atlantiki na Pasifiki zinagusana pwani za Urusi.",
"Bahari ya Karibi\nBahari ya Karibi ni bahari ya pembeni ya Atlantiki iliyoko kusini ya Ghuba ya Meksiko. Upande wa magharibi imepakana na Amerika ya Kati, kusini na Amerika ya Kusini. Pinde la Visiwa vya Karibi linaitenga na Atlantiki yenyewe.",
"Atlantiki\nAtlantiki inafunika sehemu za mabamba ya gandunia ya Amerika ya Kaskazini, Amerika ya Kusini, Karibi, Afrika na Ulaya-Asia. Yanapokutana katika ya beseni uko mgongo kati wa Atlantiki ambao ni safu ya milima chini ya bahari. Mahali pachache inafikia hadi uwiano wa bahari na kuonekana kama visiwa."
] | 6
|
Kenya ilipata Uhuru mwaka upi?
|
[
"Uchumi wa Kenya\nMiaka kumi na tano ya Uhuru wa Kenya, kama ilivyokua miaka iliyopelekea uhuru, ilitawaliwa na sifa zilizomhusu Jomo Kenyatta miongoni mwa watu. Utawala wa Kenyatta uliofikia kikoma mnamo Agosti 1978, wakati kitabu hiki hakijakamilika, unaelezewa kwa ufasaha na. Kinaelezea mchango aliokuwanao Rais huyo katika muelekeo wa Kibepari (capitalist) na kijamaa (socialist) unaodhihirika katika mikakati ya kiuchumi nchini Kenya hivi sasa.\nUshawishi wa ari ya “kinyakuzi” enzi za Kenyatta ulikuwa na athari zake. Jomo Kenyatta, muasisi wa Taifa la Kenya atakumbukwa daima kwa mchango wake katika kupatikana kwa uhuru nchini mwake. Hata hivyo, inasemekana kuwa uhuru wa Kenya ulikuja na matatizo chungu mzima: Ukabila, Rushwa, na Choyo. Nafasi za kiutawala zilipatikana kwa wachache waliokuwa na madhumuni ya kukusanya Utajiri mkubwa kadiri iwezekanavyo. Hata hivyo, mtizamo huu wa jinsi hali ilivyokuwa, unakingana na jinsi hali halisi ilivyokuwa. Je? Hakukuwa na ukabila kabla ya uhuru? Kiukweli, Jomo Kenyata hakuwa muanzilishi, bali mdhibiti mkuu wa hali ya kikabila nchini humo. Ulikuwepo na bado upo japo kuwa unadhihirika katika ngazi fulani fulani. Miezi ya mwanzo ya utawala wa Rais Daniel Arap Moi, ilitawaliwa na bidii za dhati za kutaka kuondoa makosa yote yaliyojidhihirisha katika utawala uliotangulia na kwa bahati mbaya, ulikuwa ni wakati mbaya na mgumu kiuchumi nchini Kenya. Hata hivyo, mawazo ya kuwa matatizo yote yangeweza kuisha kufumba na kufumbua, yalikosa msingi pamoja na uzuri wa matokeo yaliyokusudiwa na kwamba ukabila na rushwa ambavyo hupatikana ulimwenguni kote, vingeweza kupotea. Ni rahisi sana kulaumu nyakati zilizopita kuwa ni sababu ya matatizo ya sasa na ni rahisi pia kufikiri kuwa mambo mazuri yanaweza kupatikana kwa haraka. Kukubali matatizo yaliyouandama uongozi wa Kenyatta, sio kukataa mazuri yalo ambatana nao. Hatua kubwa zilipigwa kimaendeleo ya jamii ya watu wa Kenya miaka kumi na tano baada ya uhuru, bila kuzingatia baadhi ya maandiko yanayoweza kuwa yameandikwa nchini Kenya na kitabu hiki, kinalenga kutoa ukweli na uhalisia wa mambo.",
"Historia ya Kenya\nLicha ya Waingereza kuwa na matumaini ya kuwapa wapinzani Waafrika mamlaka \"ya wastani\" zaidi, ilikuwa Kenya African National Union (KANU) ya Jomo Kenyatta, mwanachama wa kabila la Kikuyu na mfungwa wa zamani, ambayo iliunda serikali muda mfupi kabla ya Kenya kupata uhuru tarehe 12 Desemba 1963."
] |
[
"Uhuru Kenyatta\nUhuru Muigai Kenyatta (amezaliwa 26 Oktoba 1961) ni mwanasiasa nchini Kenya ambaye amekuwa rais wa nne na wa sasa wa Jamhuri ya Kenya. Baada ya kuongoza nchi, ameshinda uchaguzi mkuu wa Agosti 2017 lakini mahakama kuu ikaamua na kuamuru na kudai urudiwe, marudio ambayo licha ya kujiondoa kwa mpinzani wake mkuu Raila Odinga, Kenyatta aliibuka mshindi kwa asilimia tisini na nane. Hatimaye alitangazwa rasmi kuwa mshindi na kuapishwa kwa kipindi chake cha pili kwa mujibu wa sheria.",
"Orange Democratic Movement\nKatika mwaka wa 2007 muungano huu ulianza kutokuwa imara, ambapo makundi mengine yalijiondoa. Chama cha Uhuru Kenyatta KANU ndicho kwanza, kujiondoa mwezi wa Julai mwaka wa 2007 na kuunga kuchaguliwa tena kwa Rais Kibaki , ingawa baadhi ya wanasiasa binafsi kutoka KANU walibaki katika ODM. kutokana nakutoelewana kati ya Kalonzo Musyoka na Raila Odinga, chama cha ODM kiligawanyika katika makundi mawili katika katikati mwa mwezi wa August2007.. Kundi la Raila, ambayo pia ni pamoja naMusalia Mudavadi, William Ruto, Joseph Nyagah na Najib Balala walijiondoa kayika ODM Kenya kuchukua chama cha ODM ambacho kilisajiliwa na Mugambi Imanyara, wakati huo kundi la Kalonzo, likiongozwa na yeye mwenyewe na Dr Julia Ojiambo llibakia katika asili ODM - Kenya.",
"Majeshi ya Ulinzi ya Kenya\nVikosi vya Uingereza vilitoka nchini tarehe 12 Disemba 1964 baada ya makubaliano yaliyofanywa tarehe 3 Juni 1964 kati ya Kenya na Katibu wa Dola kwa Uhusiano wa Jumuia ya Madola. Uingereza ilikuwa isaidie jeshi, iifadhili na itoe mafunzo kwa kikosi kipya cha Jeshi la Anga la Kenya na itengeneze Jeshi la Wanamaji la Kenya. Pia, ilikuwa itoe vitengo vya Jeshi la Kifalme la Hewani na vya Jeshi la Ardhi kuongeza usalama katika eneo la Mashariki Kaskazini. Mikopo muhimu ilikuwa ifutwe, na mali nyingi ikabidhiwe kwa Serikali ya Kenya. Kwa upande wao, ndege kutoka Uingereza zingeweza kupitia Kenya, meli za vikundi vya manowari vya Mashariki ya Mbali na vitengo vingine vya Jeshi la Kifalme la Wanamaji vingeweza kutembelea Mombasa, vifaa vya mawasiliano vingeweza kutumika hadi mwaka 1966, na vikosi vingeweza kufanya mazoezi nchini Kenya mara mbili kwa mwaka. Vikosi vya mafunzo viliendelea kutumwa nchini hadi mwaka 2015, vikisimamiwa na Kitengo cha Jeshi la Mafunzo cha Uingereza Kenya.",
"National Development Party of Kenya\nLakini katika Oktoba 2007 farakano kubwa likatokea ndani ya KANU baada ya rais Moi kumteua Uhuru Kenyatta kama mfuasi wake. Raila aliondoka katika KANU akifuatwa na kundi lake la NDP ya awali. Kundi ka NDP liliondoka pamoja na wanaKANU waliosikitika uteuzi wa Uhuru Kenyatta.",
"Uhuru Kenyatta\nKatika Novemba 2006 Biwott alirudia jaribio la kumpindua Uhuru kwa kuita mkutano wa Kanu mjini Mombasa bila idhini ya mwenyekiti wala kamati ya chama. Hapo alichaguliwa kuwa mweyekiti mpya. Kwa msaada wa serikali Biwott alifaulu kuandikisha kamati yake kama uongozi rasmi, na hivyo kumwondoa Uhuru katika nafasi ya kiongozi wa upinzani bungeni.",
"Musalia Mudavadi\nKatika uchaguzi wa urais nchini Kenya mwaka 2002, Mudavadi alikuwa ni mgombea mwenza wa Uhuru Kenyatta. Pamoja na kuungwa mkono na rais aliyekuwa akimaliza muda wake, Moi, na mtandao mkubwa wa KANU, Kenyatta na Mudavadi walishindwa uchaguzi, Kenyatta hakuchaguliwa kuwa rais na Mudavadi alipoteza kiti cha ubunge wa Sabatia.",
"Kenya\nKatika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 27 Desemba 2007, Rais Kibaki wa chama cha Party of National Unity (PNU) aliwania uchaguzi dhidi ya chama kikuu cha upinzani Orange Democratic Movement (ODM). Kulingana na wachunguzi wa kimataifa, uchaguzi huo ulikumbwa na udanganyifu na hivyo kutofikia kiwango kinachokubalika kimataifa. Chama cha ODM kilisambaratika na kupoteza 8 % ya kura zake kwa chama kipya cha Orange Democratic Movement-Kenya (ODM) - kikiongozwa na Kalonzo Musyoka. Kinyang’anyiro kilikuwa kikali kati ya mgombea wa ODM, Raila Odinga na Kibaki wa PNU. Kuhesabiwa kwa kura na Tume ya Uchaguzi ya Kenya kulionyesha Raila akiongoza kwa kura chache na baadaye kwa kura nyingi. Hata hivyo, kura zilipoendelea kuhesabiwa na Tume ya Uchaguzi, Kibaki alimkaribia mpinzani wake kwa kura, kisha akamshinda. Matokeo hayo yalisababisha maandamano na kulaumiwa kwa Tume ya Uchaguzi ya Kenya kwa kumpendelea Kibaki,hivyo Oginga akajitangaza “rais wa watu” na kutaka kura zihesabiwe tena.",
"Uchaguzi Mkuu wa Kenya, 2007\nBaada ya Raila Odinga wa ODM kuongoza katika hesabu ya kura kwa muda mrefu Tume ya Uchaguzi ya Kenya lilisimamisha hesabu ya kura kwa muda wa usiku mmoja na baada kuanza upya kura za Mwai Kibaki wa PNU zilikuwa mbele. Tume ikamtangaza Kibaki kuwa mshindi aliyeapishwa mara moja bila kusubiri muda wa kisheria kwa malalamiko. Watazamaji waliona kasoro, makosa na matokeo yaliyodokeza ya kwamba hesabu ya kura ilibadilishwa kwenye ngazi za kupiga jumla za kura kimkoa na kitaifa. Vilevile kuna madokezo ya kwamba kura za kiraisi ziliongezwa katika usiku ambako hesabu ilisimamishwa.",
"Kenya\nMswada wa ubinafsishaji umeidhinishwa ingawa kuanzishwa kwa tume ya ubinafsishaji hakujakamilika, mabadiliko katika utendakazi wa umma yametekelezwa na mwaka wa 2007 Kenya ilishinda tuzo la Umoja wa Kimataifa la Utendakazi wa Umma. Hata hivyo, kazi nyingi zinahitajika kufanywa ili kuiwezesha nchi hii kuyafikia mataifa yaliyoendelea sana kiuchumi, hasa yale ya Mashariki ya Mbali. Changamoto kuu ni pamoja na kuchukua hatua thabiti dhidi ya ufisadi, kupitisha sheria zinazoshughulikia ugaidi na biashara haramu, kutatua upungufu wa ufadhili wa bajeti kisha kurekebisha na kuunda miundo msingi. Inaaminika haya yatasaidia kudumisha sera za kimsingi za kiuchumi, na kuhakikisha ukuaji wa kasi wa kiuchumi uliofikia asilimia 7.2 mwaka wa 2007."
] | 18
|
Je mlima mkubwa zaidi nchini Uganda ni gani?
|
[
"Elgon (mlima)\nElgon ni mlima mkubwa wa pili nchini Kenya baada ya Mlima Kenya. Upande wa Uganda ni mlima mkubwa wa mashariki ya nchi lakini milima ya safu ya Ruwenzori ni mirefu kushinda Elgon."
] |
[
"Mlima Gessi\nMlima Gessi ni mlima wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wa Uganda (Afrika).",
"Wasuba (Kenya)\nMtegi ni mototo mwingine wa Girango, na walitoka Uganda sehemu ya Kitgum na wakatembea mpaka Karachuonyo. Na hapo walikaa kwa muda mrefu na wakahama mpaka nchi ya Wakipsigis. Na hapo walikaa sana, ndipo Tegi alipotengana na wenzake wakina Ongombe na Muruga. Na hapo ndipo Ongombe akahamia huko Kamagambo, ambapo hata hivi sasa bado wengi wao wanaishi huko na wanajulikana kama Wategi, \"ukoo wa Kamagambo\" au Kanyingombe. Wategi walianza kutelemka hadi wakafikia Kanyamkago na pale wakakaa kwa muda mrefu. Na kutokana na vita vya makabila walifukuzwa wakaja hadi Kanyamwa. Wategi walizidi kuja wengi kutoka huko nyuma walipokuwa wanabaki baki na wakajaa Nyandiwa na kuenea Mataro hadi Rasira Nyatambe. Mke wa Girango alikuwa binti wa Kijaluo kutoka Acholi na alizaa Gire kwao huko Kitgum–Uganda Kaskazini, kabla hajaolewa. Mke wa Girango alikuwa akiitwa \"Miluha\".",
"Milima ya Ufa Mashariki\nMilima ya Ufa Mashariki ni safu mbili za milima ya eneo la Maziwa makubwa ya Afrika, katika nchi a Kenya, Uganda, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Burundi.\nInaitwa hivyo kutokana na uhusiano wake na Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki; safu ya magharibi ina: Milima ya Virunga, Milima ya Mitumba na Milima ya Rwenzori, wakati ile ya mashariki ina vilele vya juu zaidi katika bara zima la Afrika: Mlima Kilimanjaro (mita 5,895, sawa na futi 19,340) na Mlima Kenya (mita 5,199, futi 17,058). Kati ya milima mingine kuna Mlima Elgon kati ya Kenya na Uganda. Yote, isipokuwa Ruwenzori ina asili ya volkeno.",
"Mlima Emin\nMlima Emin ni mlima wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wa Uganda (Afrika).",
"Wagadugu\nMji ni pia kitovu cha usafiri na mawasiliano. Kuna kiwanja cha kimataifa cha ndege na njia ya reli kwenda Abidjan (Côte d'Ivoire), halafu barabara za kwenda Lome (Togo), Bamako (Mali), Niamey (Niger), Accra (Ghana).",
"Mbale\nMbale ni mji wa Uganda ya kusini-mashariki mwenye wakazi 76,000 kwenye mguu wa mlima Elgon. Ni makao makuu ya wilaya ya Mbale. Umbali na Jinja ni 120 km na 190 km na Kampala.",
"Ring'wani\nKepteni, Faustine Maro Ruge ni mwanajeshi mstaafu wa JWTZ akiwa amewahi kuwa kamanda mwandamizi na mkuu wa vikosi mbalimbali nchini Tanzania. Tanzania ikiwa moja ya nchi za mstari wa mbele Ruge alipata fursa ya kushiriki kikamilifu katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika akihusika katika kufundisha wapigania uhuru hasa wa FRELIMO na ZANU PF na hata kushiriki na kuongoza harakati za siri za kijeshi na mapambano katika mataifa mbalimbali yakiwamo Msumbiji, Angola, Afrika Kusini, Komoro, Shelisheli, Namibia, Zimbabwe na Uganda aliposhiriki kwa nguvu katika harakati za kumwondoa madarakani aliyekuwa dikteta wa nchi hiyo Idd Amin Dada, ambapo pia alibaki katika kazi maalumu ya kuilinda nchi hiyo hadi mwaka 1982. Ruge ametunukiwa medani mbalimbali za utumishi uliotukuka ikiwamo nishani ya vita (Medal for Victory in Uganda), Nishani ya Kagera, Nishani ya Zimbabwe, Nishani ya Ujasiri na nyingine kadhaa, Ruge ni mmoja kati ya askari wawili wa kwanza wakati wa vita vya Kagera walioshuhudia na kuthibitisha kuwa daraja la Kagera llimevunjwa na askari wa Idd Amin, Ruge ndiye kamanda aliyeongoza zoezi la kufungua vyumba vya mateso vya dikteta Idd Amin na kuachilia huru wafungwa wengi wa kisiasa mara baada ya kuiokomboa Uganda na baadaye Ruge alipewa kazi maalum ya kulinda kituo cha kurushia matangazo cha Radio Uganda (Radio Uganda Transmitting Station). Baade Ruge alirudishwa Ikulu ya Entebbe kwa kazi ya kulinda Ikulu ya nchi hiyo na kuhakikisha usalama wa marais Godfrey Lukongwa , Yusuf Kironde na Paul , baadae yeye na wenzake walisimamia uchaguzi wa kwanza nchini Uganda baada ya kumwondoa madarakani Dikteta Idd Amin, uchaguzi huo ambao ulifanyika mwaka 1980 ulikuwa na ushindani mkali kati ya Bwana Paul na Sir. Milton , uchaguzi huo uligubikwa na utata ulioepelekea machafuko baada ya Sir. Milton Apollo Obote aliyekuwa Rafiki mkubwa wa Nyerere kutangazwa mshindi, machafuko hayo yalisababisha vifo vingi vya askari wa Tanzania hali iliyopelekea Ruge kupewa kazi maalum ya kutuliza na kukomesha maasi hayo katika jiji la Kampala na Entebbe.",
"Kongo (mto)\nHadi sasa kuna takriban vituo 49 vinayvozalisha umememaji katika beseni ya Kongo. Kituo kikubwa iko kwenye Lambo la Inga takriban kilomita 200 upande wa kusini magharibi ya Kinshasa. Mradi ulianzishwa katika miaka ya 1970. Wakati ule mfululizo ya malambo 5 ulipangwa. Hadi sasa 2 yamejengwa, lambo la kwanza Inga I ilikuwa tayari mwaka 1972, Inga II ikafuata 1982 na yote miwili ina rafadha 14 zinazoweza kuzalisha megawati 1,775 kwa jumla lakini kutokana uhaba wa matengenezo na usimamzi yanafikia si zaidi ya nusu.",
"Jiografia ya Kenya\nEneo hili la milima ndilo la juu zaidi nchini Kenya (na la pili kwa urefu barani Afrika): Mlima Kenya, unaofikia urefu wa mita 5,199 (futi 17,0570) na ni eneo lenye mito ya barafu. Ng'ambo ya mpaka wa Tanzania Mlima Kilimanjaro () huweza kuonekana upande wa kusini."
] | 48
|
Je,Burundi ilpata uhuru mwaka upi?
|
[
"Historia ya Afrika\nKatika mwaka wa 1962 Algeria, Burundi, Rwanda, na Uganda zikawa huru, na 1963 zikafuatia Zanzibar, Gambia na Kenya, na katika mwaka wa 1964 Malawi (Nyasaland), na Zambia (Rhodesia ya Kaskazini) zikapata uhuru."
] |
[
"Burundi\nTangu mwaka 1946 Shirikisho la Mataifa lilikwisha na Ubelgiji ilipokea wito wa kutawala Ruanda-Urundi na Umoja wa Mataifa. \nMwaka moja kabla ya uhuru kulikuwa na uchaguzi wa kwanza chini ya usimamizi ya UM na chama mshindi kilikuwa UPRONA kilichoongozwa na mwanamfalme Mtutsi Louis Rwagasore aliyemwoa mwanamke wa Kihutu na chama kiliunganisha pande zote mbili. Lakini miezi michache baadaye Rwagasore aliuawa na chama chake kilitengana kufuatana na ukabila.",
"Historia ya Burundi\nKatika hali hiyo Burundi ilikaribia [[uhuru]]. [[Chama cha siasa|Vyama vya siasa]] viliundwa vilivyofuata ugawaji wa kimbari kati ya Watutsi na Wahutu. Mapigano ya kwanza kati ya Wahutu na Watutsi yalitokea mwaka [[1959]] kabla ya uhuru yakakomeshwa na Wabelgiji.",
"Historia ya Burundi\nMwaka moja kabla ya uhuru kulikuwa na uchaguzi wa kwanza chini ya usimamizi ya [[UM]] na chama mshindi kilikuwa UPRONA kilichoongozwa na mwanamfalme Mtutsi [[Louis Rwagasore]] aliyemwoa [[mwanamke]] wa Kihutu na chama kiliunganisha pande zote mbili. Lakini miezi michache baadaye Rwagasore aliuawa na chama chake kilitengana kufuatana na ukabila.",
"Historia ya Burundi\nBaada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Burundi pamoja na Rwanda ilikabidhiwa kwa Ubelgiji kwa niaba ya Shirikisho la Mataifa kama [[eneo la kudhaminiwa] lililoitwa Ruanda-Urundi. Kimsingi Wabelgiji waliendelea na mfumo wa Wajerumani uliomwachia mtemi [[mamlaka]] kubwa. Waliweka Ruanda-Urundi chini ya serikali ya Kongo ya Kibelgiji.",
"Burundi\nMwaka 1966 mwami alipinduliwa na mwanasiasa Michel Micombero aliyejitangaza kuwa rais na nchi kuwa jamhuri. Kuanzia hapo wanasiasa na watumishi wakubwa walio Wahutu walifukuzwa, kukamatwa au kuuawa.\nBurundi ilundwa kama ufalme ulioongozwa na Watutsi waliotawala Wahutu. Lakini kabla ya ukoloni mipaka kati ya makundi hayo haikuwa imara mno; Wahutu matajiri katika utumishi wa mwami waliweza kupanda ngazi na kuwa Watutsi na pia Watutsi maskini waliweza kushuka ngazi na kuhesabiwa kati ya Wahutu, hasa baada ya kuoa au kuolewa na mtu wa upande mwingine. Uhusiano wa makundi hayo ulifanana zaidi na ule wa matabaka si wa makabila tofauti, pia kwa sababu lugha ilikuwa moja kwa wote.",
"Historia ya Burundi\nBurundi ilundwa kama ufalme ulioongozwa na Watutsi waliotawala Wahutu. Lakini kabla ya ukoloni mipaka kati ya makundi hayo haikuwa imara mno; Wahutu ma[[tajiri]] katika utumishi wa mwami waliweza kupanda ngazi na kuwa Watutsi na pia Watutsi [[maskini]] waliweza kushuka ngazi na kuhesabiwa kati ya Wahutu, hasa baada ya [[Ndoa|kuoa]] au kuolewa na mtu wa upande mwingine. Uhusiano wa makundi hayo ulifanana zaidi na ule wa [[tabaka|matabaka]] si wa makabila tofauti, pia kwa sababu lugha ilikuwa moja kwa wote.",
"Historia ya Burundi\nKipindi kilichofuata kilikuwa cha [[Vita ya wenyewe kwa wenyewe]] katika sehemu mbalimbali za nchi. \n[[Picha:BujumburaAirport.jpg|300px|thumbnail|Uwanja wa Ndege, Bujumbura]]\nTangu mwaka [[1995]] [[Umoja wa Afrika]] na [[Umoja wa Mataifa]] zilijitahidi kujenga mapatano kati ya vikundi. Marais na [[wanasiasa]] walioshiriki katika [[jitihada]] hizo walikuwa pamoja na [[Julius Nyerere]], [[Boutros Boutros-Ghali]], [[Nelson Mandela]], [[Thabo Mbeki]] na rais wa [[Marekani]] [[Bill Clinton]].",
"Robert Mugabe\nMara baada ya uchaguzi tu mwezi Novemba 1980 Mugabe alianza kampeni ya kuua kwa wingi watu wa kabila la wa-Ndebele ambao mjia wao mkubwa unaitwa Bulawayo. Ingawa mauaji hayo hayakufikia kiwango cha yale ya Rwanda na Burundi, waliuawa wanawake, wanaume, watoto na hata vichanga vilivyokuwa matumboni. Mwaka 1981 pia Mugabe aliendelea kuua wandebele tukio ambalo halikutangazwa sana na vyombo vya habari. Kuanzia enzi hizo hadi leo raisi Mugabe amejaribu kushinda kila uchaguzi unaokuja nchini huko kwa kutumia nguvu za kikabila na mabavu.",
"Patrice Lumumba\nMaadhimisho ya uhuru wa Congo kwa mara ya kwanza yalifanyika mnamo tarehe 30 June 1960 ambapo maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na Mfarme Baudouinwa Ubeljiji pamoja na vyombo mbalimbali vya habari kutoka nchi za nje. Lumumba alitoa hotuba yake kama Waziri mkuu katika nchi huru japo yeye alikuwa ameenguliwa katika ratiba ya shughuli hiyo. Hotuba ya Mfalme wa Ubeljiji Mfalme Baudouin alihutubia kwa kutukuza utawala wa kikoloni, huku akilingania fikra za mjombae ambae alikuwa mfalme wa Ubeljiji akiitwa Léopold wa Pili glossing over atrocities committed during the Taifa huru la congo. Mfalme aliendelea kutoa masharti, \"aliwataka kuto kufanya mabadiliko yoyote mpaka hapo wao watakapo ona kwamba wanaweza kufanya vyema, na kwamba hawakutakiwa kufanya mabadiliko yoyote yalika bidhiwa na kwamba tutaendelea kutoa ushauri. \" Lumumba aliufahamisha umma kwamba uhuru uliotolewa na wabeljiji sio haukuja hivihivi:",
"Historia ya Burundi\nKatika Burundi kikosi cha kwanza cha Kijerumani kilifika mnamo 1896 wakakuta ufalme wa mwami wakaridhika kumwacha mwakilishi mkazi (resident) katika mji mkuu Gitega ambaye hakuhusika na mambo ya utawala wa ndani. Wakati ule eneo lilijulikana kwa jina \"Urundi\". Hapa sawa na Rwanda na Bukoba Wajerumani walitumia mbinu ya eneo lindwa ingawa walikuwa pia na majadiliano kuingiza falme hizi za kienyeji moja kwa moja ndani ya koloni lao."
] | 18
|
Je,Kenya ina vyama ngapi vya kisiasa kufikia mwaka 2019?
|
[
"Orodha ya vyama vya kisiasa nchini Kenya\nKenya ilikuwa na vyama vya kisiasa vilivyosajiliwa zaidi ya 160 kufikia mwezi Novemba mwaka wa 2007 lakini kufuatia kupitishwa kwa sheria maalum ya vyama vya siasa tarehe 31 Desemba 2008, idadi ya vyama vilivyoandikishwa ilipungua hadi 38 huku vyama kadhaa vikiongezewa muda wa kujilinganisha na sheria hii mpya."
] |
[
"Ruwaza ya Kenya 2030\nRuwaza ya Kenya 2030 (Kiingereza: \"Kenya Vision 2030\") ni mpango wa maendeleo ya kiuchumi wa serikali ya Kenya kuendeleza maeneo mbalimbali ya kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya nchi. Malengo ya mpango kuzalisha ukuaji wa uchumi wa mwaka wa 10%. Hivi sasa, Kenya ina ukuaji wa Pato la Taifa 4.9% (2007). Maono haya yamefululizwa katika miaka mitano mitano ya mipango, mwanzo wake ukiwa 2008-2012. Mpango wa kwanza unaazimia uwekezaji katika sekta sita muhimu na miradi ishirini kabambe . Sekta zilizolengwa ni pamoja na utalii, kilimo, viwanda, biashara, teknolojia ya habari, na huduma za kifedha.",
"Kenya African National Union\nKatika uchahguzi wa 1963. KANU ilishinda vyama vya KADU na APP na kupata ruhusa ya kuunda serikali huru ya kwanza nchini Kenya. Mwaka iliyofuata wabunge wa hivi vyama walivuka sakafu na kujiunga na KANU. Kenya ikawa nchi ya utawala wa chama kimoja, yaani defacto. Mambo yaliendelea hivo hivo, isipokuwa muda mfupi kutoka 1966-69, mpaka 1982 mwaka katiba ya Kenya iliharirishwa kulingana na mfumo wa chama kimoja na KANU kuwa chama cha kisiasa cha pekee yaani dejure. Vyama vingine vilipigwa marufuku. Hali hii ilidumu hadi 1991 wakati serikali ya Moi ililazimishwa kukubali vyama vingi na badiliko la katiba tena.",
"Katiba ya Kenya\nRasimu ya katiba ya 2010 iliandikwa na Kamati ya Wataalamu na kuchapishwa kwa umma tarehe 17 Novemba 2009 ili kuwezesha mjadala wa umma na bunge iamue kama ingetaka ipigiwe kura ya maoni. Umma ulipatiwa muda wa mwezi mmoja kuikagua na kupeleka mapendekezo na marekebisho kwa wabunge wao. Rasimu rekebishe ilipelekwa kwa Kamati ya Bunge ikarekebishwa na kurudishwa kwa Kamati ya Wataalamu. Waliichapisha Katiba Iliyopendekezwa tarehe 23 Februari 2010, iliyopelekwa bungeni ipigwe msasa.",
"Kenya\nMswada wa ubinafsishaji umeidhinishwa ingawa kuanzishwa kwa tume ya ubinafsishaji hakujakamilika, mabadiliko katika utendakazi wa umma yametekelezwa na mwaka wa 2007 Kenya ilishinda tuzo la Umoja wa Kimataifa la Utendakazi wa Umma. Hata hivyo, kazi nyingi zinahitajika kufanywa ili kuiwezesha nchi hii kuyafikia mataifa yaliyoendelea sana kiuchumi, hasa yale ya Mashariki ya Mbali. Changamoto kuu ni pamoja na kuchukua hatua thabiti dhidi ya ufisadi, kupitisha sheria zinazoshughulikia ugaidi na biashara haramu, kutatua upungufu wa ufadhili wa bajeti kisha kurekebisha na kuunda miundo msingi. Inaaminika haya yatasaidia kudumisha sera za kimsingi za kiuchumi, na kuhakikisha ukuaji wa kasi wa kiuchumi uliofikia asilimia 7.2 mwaka wa 2007.",
"Kenya\nWadhifa huo mpya wa waziri mkuu utakuwa na nguvu na mamlaka kuratibu na kusimamia shughuli za serikali. Vilevile itaongozwa na mbunge aliyechaguliwa ambaye pia atakuwa kiongozi wa chama au muungano wa vyama wenye idadi kubwa ya wabunge bungeni. Ulimwengu ulimshuhudia Annan na kamati yake iliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na mwenye kiti wa muungano wa nchi za Afrika Jakaya Kikwete, walipowaleta pamoja wapinzani hawa sugu kwenye sherehe za kutia sahihi mkataba huu. Sherehe hizi zilionyeshwa moja kwa moja kwenya televisheni ya kitaifa kutoka kiingilio cha Jumba la Harambee mjini Nairobi. Wawakilishi wa PNU na ODM walianza majadiliano ya kina kuhusu ugavi wa mamlaka tarehe 29 Februari 2008. Wabunge wa Kenya, kwa pamoja, waliidhinisha mkataba wa ugawaji mamlaka tarehe 18 mwezi wa Machi 2008 ili kuiokoa Kenya iliyoaminika kama mojawapo ya nchi thabiti na iliyoendelea barani Afrika. Mkataba huu uliunganisha PNU iliyoongozwa na Kibaki na ODM ya Odinga kisha kupelekea kuundwa kwa serikali ya muungano, vyama vyote viwili vikiwa na mamlaka sawa.",
"Historia ya Kenya\nUchaguzi wa vyama vingi vya kisiasa wa Desemba 1992 ulimpa Rais ushindi chini ya chama cha KANU kwa kupata viti vingi. Rais Moi alichaguliwa tena kwa muda wa miaka mitano, ingawa vyama vya upinzani vilishinda asilimia 45 ya viti vya bunge. Harakati ya demokrasia ya Kenya ilivunjika kabla ya uchaguzi, hivyo basi kuisaidia KANU kubaki madarakani.",
"Seneti ya Kenya\nMwaka wa 2013, uchaguzi wa Seneti ulifanyika tarehe 4 Machi 2013. Chini ya katiba mpya, ambayo ilipitishwa wakati wa kura ya maoni ya mwaka 2010, uchaguzi mkuu wa 2013 ndio ulikuwa wa kwanza kujumuisha Maseneta wanaowakilisha kaunti 47. Ulikuwa pia uchaguzi mkuu wa kwanza wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).",
"Uchaguzi Mkuu wa Kenya, 2007\nWabunge 207 walichaguliwa. Kura zitarudiwa katika majimbo 3. Wabunge 12 wa ziada watateuliwa na rais. Akifuata kawaida atawateua kufuatana na nguvu ya vyama bungeni.Magazeti yalitoa taarifa ya kwamba wabunge 30 wa vyama vidogo waliunda \"Kundi la vyama vidogo bungeni\" (Small Parties Parliamentary Group); idadi hii ingejumlihsa wabunge waliohesabiwa juu kama kundi la PNU.",
"Uchaguzi wa bunge nchini Kenya, 2007\nBunge la 9 la Kenya lilivunjwa mnamo Jumatatu 22 Oktoba, 2007 Tarehe rasmi ya uchaguzi, ilivyotangazwa na rasmi mnamo 26 Oktoba 2007 na Tume ya Uchaguzi ya Kenya (ECK), ingekuwa Alhamisi tarehe 27 Desemba 2007. Hii ilimwezesha Spika wa bunge kutoa idhinisho kwa wabunge kuondoka ofisini, hivyo kutangaza nafasi 210 za wabuge wazi. Kisha ECK ilitangaza tarehe ambayo uchaguzi mkuu ungefanyika. Ilivyo kawaida, Wagombezi wanatakiwa kuteuliwa katika chochote kati ya vyama 144 vilivyosajiliwa ili wahitimu kuwa katika uchaguzi. Idadi ya wengi inahitajika kushinda uchaguzi wa bunge. Washindi watakuwa wabunge wateule hadi sherehe rasmi ya kuapishwa kwa Bunge la kumi."
] | 11
|
Bergisch Gladbach ina idadi ngapi ya watu?
|
[
"Bergisch Gladbach\nBergisch Gladbach ni mji uliopo nchini Ujerumani katika jimbo la Rhine Kaskazini-Westfalia. Mji upo karibu na mji wa Cologne na una wakazi takriban 110,016 waishio katika mji huo."
] |
[
"Bergisch Gladbach\nMakazi ya awali yalianza tangu kunako karne ya 13, lakini mji ulitambuliwa rasmi mnamo mwaka wa 1856. \nNeno “Bergisch” linatokana na asili ya eneo lake la Berg na ulipangwa kuondolewa katika Mönchengladbach. Mnamo mwaka wa 1975, mji huu ukishirikiana na mji wa jirani yake wa Bensberg na ulipofikia idadi ya watu 100,000 mnamo 1977 ukapewa heshima kuwa jiji.",
"Bergheim\nBergheim ni mji wa Rhine Kaskazini-Westfalia nchini Ujerumani. Idadi ya wakazi wake ni takriban 62.143.",
"Bergisch Gladbach\nMji wa Bergisch Gladbach upo mjini mashariki mwa Mto Rhine, kilomita kumi mashariki kwa mji wa Cologne.",
"Breinigerberg\nBreinigerberg ni kitongoji chenye wakazi 971 ambacho ni sehemu ya mji wa Stolberg (karibu na Eschweiler) uliopo baina ya Köln na Aachen karibu na Uholanzi na Ubelgiji.",
"Gladbeck\nGladbeck ni mji wa Rhine Kaskazini-Westfalia nchini Ujerumani. Idadi ya wakazi wake ni takriban 75.520.",
"Bremen\nBremen ni mji mwenye bandari muhimu katika Ujerumani ya Kaskazini. Iko kando ya mto Weser takriban 50 km kabla haujaingia katika Bahari ya Kaskazini. Ina wakazi 546,000. Pamoja na eneo la jirani kuna watu milioni 2.37 katika mazingira ya Bremen. Weser inapanuka baada ya kupita mji kuwa na mdomo pana sana kabla ya kuishia baharini hivyo meli zinaweza kufika hadi mjini.",
"Arnsberg\nArnsberg ni mji wa Rhine Kaskazini-Westfalia nchini Ujerumani. Idadi ya wakazi wake ni takriban 74.805.",
"Bergisch Gladbach\nKwa kuanzia kaskazini mwa mji huu, miji ya jirani na mji huu ni: Odenthal, Kürten, Overath, Rösrath, Cologne na Leverkusen."
] | 13
|
Rais wa kwanza wa Ethiopia aliitwa nani?
|
[
"Historia ya Ethiopia\nSerikali ya Majimbo ya Demokrasia ya Jamhuri ya Ethiopia ilichukua mamlaka mnamo Agosti 1995. Rais wa kwanza Negasso Gidada. EPRDF ikaongoza serikali na Waziri Mkuu Meles Zenawi ambaye ameunga mkono majimbo ya kikabila, na kuwapa madaraka viongozi wa kikabila. Ethiopia sasa ina maeneo 9 ambayo yana serikali ya madaraka ya shirika, na hata majimbo haya yanakubaliwa kutoza ushuru na kutumia akiba ya ushuru. Hii aina ya serikali imefanya Waethiopia kupata uhuru wa siasa lakini Uhuru wa idhaa na gazeti bado umefinyiliwa.",
"Ethiopia\nSerikali ya Majimbo ya Demokrasia ya Jamhuri ya Ethiopia ilichukua mamlaka mnamo Agosti 1995. Rais wa kwanza Negasso Gidada. EPRDF ikaongoza serikali na Waziri Mkuu Meles Zenawi ambaye aliunga mkono majimbo ya kikabila, na kuwapa madaraka viongozi wa kikabila. Ethiopia sasa ina majimbo 9 ambayo yana serikali ya madaraka ya shirika, na hata majimbo haya yanakubaliwa kutoza ushuru na kutumia akiba ya ushuru. Hata hivyo, uhuru wa habari na kisiasa bado umefinywa."
] |
[
"Ellen Johnson-Sirleaf\nJohnson amekuwa Rais wa kwanza mwanamke barani Afrika. Hata hivyo yeye sio mwanamke wa kwanza kuongoza nchi barani Afrika. Malikia Zauditu wa Ethiopia aliongoza nchi yake kwa miaka 13 toka mwaka 1917 hadi 1930. Ruth Perry ni mwanamke wa kwanza Afrika kuwa mkuu wa nchi pale alipokuwa mwenyekiti wa urais wa pamoja wa jamhuri ya Liberia toka mwaka 1996 hadi 1997.",
"Zauditu wa Ethiopia\nZauditu (29 Aprili 1876 – 2 Aprili 1930) alikuwa malkia mtawala wa Uhabeshi kuanzia 27 Septemba 1916 hadi kifo chake. Alimfuata Iyasu V. Jina lake la kubatizwa lilikuwa \"Askala Maryam\". Alikuwa mtoto wa kwanza wa Menelik II. Mwanzoni utawala wake ulisumbuliwa na uasi wa Iyasu aliyekuwa ameuzuliwa. Malkia huyu anajulikana kwa jinsi alivyopenda dini na alivyokuwa mpinzani mkubwa wa mabadiliko aliyokuwa akiyafanya Ras Tafari Makonnen. Zauditu aligombana sana naye Makonnen, kuhusu mambo ya siasa lakini alishindwa. Naye Tafari alimfuata kama mfalme chini ya jina la Haile Selassie.",
"Ethiopia\nSerikali ya Zenawi ilichaguliwa tena mwaka 2000 kwa uchaguzi wa kwanza wa Kidemokrasia, Rais akiwa Girma Wolde-Giorgis.",
"Historia ya Ethiopia\nUchaguzi wa Ethiopia uliendekeza wanabaraza kwa viti 547 Bungeni. Baraza hilo la bunge lilijumuika Juni 1994 na kupitisha katiba mpya ya Jimbo la Demokrasia ya Jamhuri ya Ethiopia mnamo Desemba 1994. Uchaguzi huu ulikuwa wa kwanza kuchagua wanabaraza wa kitaifa kwa sifa bungeni na wanabaraza wa majimbo mnamo Mei na Juni 1995. Vyama vingi vya upinzani viligoma kushiriki uchaguzi. Ushindi ulichukuliwa na Chama cha Mapinduzi cha Kidemokrasi cha Watu wa Ethiopia (EPRDF). Umoja wa Mataifa ukasema vyama vya upinzani vingeweza kushiriki uchaguzi kama zingetaka.",
"Historia ya Ethiopia\nSerikali ya Zenawi ilichaguliwa tena mwaka 2000 kwa uchaguzi wa kwanza wa Kidemokrasia, Rais akiwa Girma Wolde-Giorgis.",
"Simeon Nyachae\nNyachae alistaafu kutoka kwa utumishi wa umma mnamo mwaka wa 1987 akaanza kujenga maisha yake ya kisiasa. Katika mwaka 1992 alichaguliwa mara ya kwanza kama mbunge wa Nyaribari Chache na Rais Moi akamteua kuwa Waziri wa Kilimo. Mwaka wa 1997 akawa Waziri wa Fedha. Mwaka mmoja baadaye, Rais Moi alimteua kama Waziri wa Usitawi na Nyachae akakataa na kujiuzulu kama Waziri na pia kutoka chama cha KANU, na akjiunga na Ford-People, chama kidogo cha upinzani, kilicho na ushawishi wa wanasiasa wa kutoka katika mkoa wa Kati.",
"Menelik II.\nMenelik II (17 Agosti 1844 – 12 Desemba 1913) alikuwa mfalme mkuu wa Uhabeshi kutoka 1889 hadi 1913. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa \"Sahle Miriam\". Alikuwa mtemi (Ras) wa jimbo la Shoa kati ya 1865-1889. Akashinda katika mvurugo baada ya kifo cha Yohane IV kwa msaada wa Italia akakubaliwa mfalme mkuu wa Ethiopia mwaka 1889. Alikataa madai ya Italia kutokana na mkataba wa Wuchale. Mwaka 1896 alishinda jeshi la Italia katika mapigano ya Adowa. Ushindi huu ulihakikisha uhuru wa Ethiopia kama nchi ya pekee katika Afrika nje ya Liberia. Menelik aliweka misingi ya maendeleo ya Ethiopia kuwa nchi ya kisasa lakini hakubadilisha muundo wa utawala wa kimakabaila.",
"Rais wa Afrika ya Kusini\nRais anachaguliwa na wabunge wa kitengo cha chini \"(National Assembly)\" cha Bunge la Afrika Kusini. Kwa kawaida huwa kiongozi wa chama kikubwa zaidi bungeni, ambacho kimekuwa African National Congress tangu uchaguzi wa kwanza baada ya kupinduliwa kwa apartheid (ubaguzi wa rangi) uliyofanyika tarehe 27 Aprili 1994. Rais wa kwanza kuchaguliwa chini ya katiba mpya alikuwa Nelson Mandela, ambaye alifuatwa na Thabo Mbeki mwaka wa 1999, kufuatiwa na Kgalema Motlanthe mnamo Septemba 2008 na kisha Jacob Zuma mnamo Mei 2009. Katika § 5, sehemu ya 88, katiba inaruhusu wakati wa Rais ofisini kuwa muhula miwili. Marais huchaguliwa kila baada ya uchaguzi wa wabunge, na uchaguzi huu huwapa marais muda wa miaka mitano, pamoja na nafasi ya kurudishwa mara moja."
] | 56
|
Simba huzaa baada ya muda gani?
|
[
"Simba\nWengi wa simba jike huanza kuzaa wakiwa na miaka minne. Simba hawajamiani katika kipindi maalumu cha mwaka. Kama ilivyo kwa paka wengine, uume wa simba una kama miiba zilizogeukia nyuma. Wakati wa kuutoa, miiba hiyo hukwangua kuta za uke na kusababisha kuachiwa kwa yai. Akiwa kwenye joto, simba jike huweza kujamiana na zaidi ya dume mmoja, na wakati wa kujaamiana, ambao unaweza kuchukua siku kadhaa, wenza hao hujamiana mara ishirini mpaka arobaini kwa siku na mara nyingi hata huahirisha kula. Simba huzaliana vizuri kwenye hifadhi.",
"Simba\nSimba jike hubeba ujauzito kwa siku 110, na kisha hujifungua watoto mmoja mpaka wane kwenye sehemu maalumu, mara nyingi mbali na lilipo kundi lake. Mara nyingi huwinda peke yake wakati watoto bado hawajiwezi, wakikaa karibu na watoto huzaliwa wakiwa hawaoni, mpaka baada ya wiki hivi."
] |
[
"Simba Wanyika\nKutekelezwa kwa vikwazo baina ya mpaka wa Kenya-Tanzania ilisababisha watu kukua kwa muziki na kuelekea katika mtindo wa uliokuwa unajitokeza wa benga nchini Kenya. Simba Wanyika waliendelea kucheza rumba, na walikuwa bado maarufu wakati bendi ilipogawanyika katika miaka ya 1970 wakati mpiga gitaa Omar Shabini alichukua baadhi ya wanamuziki wake na kutengeneza Les Wanyika. Mwaka wa 1980, George Kinyonga pia alijiondoa katika Simba Wanyika, akachukua wanamuziki zaidi na kuunda bendi ya Orchestra Jobiso. Lakini baadaye alirudi Simba Wanyika huku bado akifanya miradi za upande na Jobiso. Simba Wanyika baadaye walibadilisha jina lao hadi \"Simba Wanyika Original\" ili kuzuia mkanganyiko na Les Wanyika na kundi lilojigawa kutoka kwao la Super Wanyika Stars.",
"Simba\nSimba hutumia muda wao mwingi wa siku kupumzika kwa takriban saa 20 kwa siku. Japokuwa wanaweza kuamka muda wowote, lakini hali hiyo hutegemea zaidi cha kuchangamana. Kipindi hicho mara nyingi baina huwa usiku mpaka mapambazuko ambako hasa ndio muda wa kuwinda. Hutumia kwa wastani saa mbili kwa siku kutembea na dakika 50 kula.",
"Kindi-miamba\nHula manyasi hasa lakini pengine matunda, mbegu na majani pia. Wana meno yenye kichwa kirefu na mizizi mirefu. Jike huzaa jozi ya watoto mara moja kwa mwaka, kiwango kidogo cha kuzaa kisicho kawaida baina ya wagugunaji. Watoto hulikizwa baada ya wiki tatu lakini waendelea kutegemea wazazi wao muda wa miezi tisa.",
"The Lion King\nSimba alikua huku akiwa shupavu kwelikweli pale alipojiunga na rafiki yake wa udogoni Nala, ambaye alikuwa akijua kwamba baba yake Mufasa yu hai. Alimweleza kuhusu mambo ya kishenzi anayoyafanya Scar na kumwomba Simba arudi ili apambane na Scar. Simba akarudi zake nyumbani na kuanza kupambana na Scar kwa ajili ya ufalme, na ikatokea Scar akaeleza ukweli kwamba yeye ndiye aliyemwua Mufasa. Kulikuwa mapigano ya muda mrefu, lakini Simba akamshinda Scar, akadai kwamba yeye ana haki ya kuwa mfalme. Nala akawa malkia wa Simba na wakazaa kitoto chao wenyewe.",
"Simba\nHuwa na uzito wa kg 1.2-2.1 wakati wa kuzaliwa na huweza kuanza kutambaa baada ya siku moja mpaka mbili na kuweza kutembea nje baada ya majuma matatu. Simba jike huyo huwahamisha watoto wake mara kadhaa kwa mwezi, kwa kuwabeba mmojammoja kwa shingo zao, ili kuzuia harufu kujijenga kwenye malazi yao na hivyo kuvuta wanyama wengine wala nyama ambao pengine wangeweza kuwadhuru watoto.",
"Simba\nSimba ni miongoni mwa wale paka wakubwa wane wa jenasi Panthera, na mmoja wa familia ya Felidae. Kwa kuwa baadhi ya simba dume wanazidi kg 250 kwa uzito, wanakuwa ndio paka wa pili kwa ukubwa baada ya tiger. . Simba wa porini wanapatikana huko nchi za Nusu-Jangwa Sahara katika Afrika na Asia na kwa kiasi kidogo sana huko India, kisha kupotea katika Afrika ya Kaskazini, Mashariki ya kati na Magharibi mwa Asia nyakati za historia. Karibu miaka 10,000 iliyopita, simba walikuwa ndio wanyama wa nchi kavu waliotawanyika zaidi baada ya binadamu. Walipatikana hasa Afrika, Mashariki mwa Ulaya mpaka Asia, na Amerika kuanzia Yukon mpaka Peru.",
"Simba\nSimba pia wana uwezo wa kushambulia wanyama wanaofugwa na binadamu; kwa mfano huko India ng’ombe wengi huwa chakula cha simba. Simba pia wanaweza kula wanyama wenzao wanaokula nyama kama vile chui, duma, fisi na mbwa mwitu. Pia wakati mwingine hula mizoga ya wanyama wengine waliouawa kwa majanga au na wanyama wengine, na huangalia sana mahali wapozungukazunguka tai, wakijua fika mahali walipo patakuwa na mizoga. Simba anaweza kula mpaka kg 30 kwa mlo mmoja; na kama hawezi kula windo lake lote, hupumzika kwa saa kadhaa na kisha kuendelea tena. Wakati wa mchana na joto kali, kundi la simba hukaa kivulini na dume mmoja au wawili kubakia kama walinzi. Simba jike anahitaji walau kg 5 za nyama kwa siku wakati dume ni kg 7.",
"Nyati wa Afrika\nMajike huzaa mara ya kwanza baada ya miaka mitano, baada ya kipindi cha mimba miezi 11.5. Ndama waliozaliwa hufichwa katika vichaka kwa wiki chache za kwanza wakitunzwa na mama zao kabla ya kujiunga na kundi kuu. Ndama huwa katikati ya kundi kwa ajili ya usalama."
] | 55
|
Tanzania ina idadi ya watu wangapi?
|
[
"Tanzania\nIdadi ya watu kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 ilikuwa 44,928,923 (nchi ya 30 duniani) kutoka 34,443,603 waliohesabiwa katika sensa ya mwaka 2002."
] |
[
"Jiografia ya Tanzania\nTanzania ina idadi kubwa sana ya watu waishio nchini, kutokana na makabila mbalimbali yaliyomo nchini, yakiwemo ya Wasukuma, Wanyamwezi, Wahaya, Waha, Wagogo, Wanyakyusa, Wahehe, Wachaga, Waluguru, Wazaramo na mengineyo.",
"Bunge la Tanzania\nMajimbo yanatofautiana kwa kiasi kikubwa katika idadi ya wakazi. Wastani ya Tanzania bara ni mbunge mmoja kwa wakazi 227,461. Kuna majimbo katika mikoa ambako mbunge mmoja anawasilisha watu wengi zaidi kama vile Dar es Salaam (wakazi 546,542/mbunge 1), Mwanza (346,999) na Kagera (309,953). Kinyume chake kuna majimbo mengine ambako mbunge anawasilisha watu wachache kama vile Pwani(wakazi 133.104/mbunge), Katavi (128.513), Njombe (120.795) au Lindi (112.192).",
"Tanzania\nWatu wa Tanzania hawaenei sawasawa. Katika maeneo makavu sana, kwa wastani kuna mtu mmoja tu kwa kilomita ya mraba (1/km²), lakini sehemu zenye rutuba za bara, kuna watu 51 kwa kila kilomita ya mraba. Hatimaye huku Unguja kuna watu 134 kwa kilomita ya mraba na katika Mkoa wa Dar es Salaam ni 3,133 kwa kilomita ya mraba.",
"Kinyamwanga\nKinyamwanga (pia huitwa \"Kimwanga\" au \"Kinamwanga\") ni lugha ya Kibantu nchini Zambia na Tanzania inayozungumzwa na Wanyamwanga. Mwaka wa 2010 idadi ya wasemaji wa Kinyamwanga nchini Zambia imehesabiwa kuwa watu 140,000. Pia kuna wasemaji 87,000 nchini Tanzania (1987). Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kinyamwanga iko katika kundi la M20.\nKitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:",
"Wabende\nWabende ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mpanda. \nMwaka 1999 idadi ya Wabende ilikadiriwa kuwa 27,000 , lakini takwimu ya mwaka 2016 inakadiria kabila la Wabende kuwa na idadi ya watu 125,000.",
"Wabondei\nWabondei ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika wilaya ya Muheza, Mkoa wa Tanga, karibu na Milima ya Usambara. Lugha yao ni Kibondei. Mwaka 1987 idadi ya Wabondei ilikadiriwa kuwa na watu 80,000 .",
"Yombo Vituka\nYombo Vituka ni jina la kata ya Wilaya ya Temeke katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania yenye postikodi namba 15115. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2002, kata ina wakazi wapatao 59,975 waishio humo.\nYombo Vituka awali kwenye miaka ya 1980 na mwanzoni mwa miaka ya 1990 ilikuwa na eneo kubwa la mashamba ya watu ya miembe, mikorosho, mpunga, na kadhalika. Lakini kuanzia miaka ya 1995 na kuendelea, kata imeanza kupanuka kwa kiasi kikubwa sana na kupelekea kuwa na majumba mengi ya watu wenye uwezo. Leo hii, Yombo Vituka imekuwa sehemu yenye wakazi wengi kupita hata kata zake za jirani kama vile Kiwalani na Kitunda.",
"Wawanda\nWawanda ni kabila la watu kutoka kusini-magharibi mwa nchi ya Tanzania. Wanapatikana katika mkoa wa Songwe, wilaya ya Mbozi, hususani tarafa ya Kamsamba maarufu kama bondeni, yenye kata za Kamsamba, Chilulumo, Mkulwe, Mpapa na Ivuna.\nMwaka 1987 idadi ya Wawanda ilikadiriwa kuwa 24,000 .",
"Afrika ya Mashariki\nTanzania, Kenya na Uganda zina ukubwa wa eneo la maili za mraba; Tanzania 360,000 ikifuatiwa na Kenya 224,960 na Uganda 93,980 upande wa mashariki nchi hizi zimepakana na bahari ya Hindi na upande wa kaskazini mashariki zimepakana na Somalia, upande wa kaskazini zimepakana na Ethiopia na Sudan Kusini upande wa magharibi ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na jamuhuri ya Rwanda na Burundi, kusini ni Zambia, Malawi na Msumbiji.",
"Mbezi\nMbezi ni jina la kata ya Wilaya ya Ubungo katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania yenye postikodi namba 16113. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ina wakazi wapatao 73414 waishio humo. Inasemekana jamii iliyokuwa na watu wengi ni Wagogo wanaopatikana sehemu za Mpiji Magoe mtaa wa Makuti kijiji cha Msakuzi."
] | 53
|
Mji mkuu wa South Sudan ni upi?
|
[
"Equatoria ya Kati, Sudan\nEquatoria ya Kati ni jimbo la Sudan Kusini. Mji mkuu ni Juba. Jimbo lilitwa \"Bahr al Jabal\" hadi mwaka 2006.",
"Sudan Kusini\nMji mkuu ni Juba, wenye wakazi 1.118.233."
] |
[
"Bahari ya Shamu, Sudan\nBahari ya Shamu al-Bahr al-Ahmar) ni moja ya Wilayat au majimbo 26 ya Sudan. Lina ukibwa wa eneo la 218,887 km ² na wakaazi wanaokadiriwa kuwa 700,000 (2000). Port Sudan ndio mji mkuu wa jimbo hili. Sudan bado inadai, lakini haina udhibiti katika Hala'ib Triangle, mkoa ambao umekuwa chini ya utawala wa Misri tangu 2000.",
"South Dakota\n\"South Dakota\"' (Dakota Kusini) ni jimbo la Marekani upande wa kaskazini kati ya nchi. Mji mkuu ni Pierre na mji mkubwa ni Sioux Falls. Imepakana na North Dakota (Dakota Kaskazini), Minnesota, Iowa, Nebraska, Wyoming na Montana. Jimbo lina wakazi wapatao 804,1974 (2008) wanaokalia katika eneo la kilomita za mraba zipatazo 199,905.",
"Khartoum\nKhartoum (الخرطوم al-Khartūm) ni mji mkuu wa Sudan na pia mki mkuu wa dola la shirikisho la Khartoum. Mji uko mahali mito ya Nile nyeupe na Nile ya buluu inapokutana. Kisheria \"Khartoum\" ni eneo tu mashariki ya Nile nyeupe na kusini ya Nile ya buluu lakini hali halisi Khartoum pamoja na miji ya Omdurman na Bahri ni kama mji mmoja mkubwa sana unaounganishwa kwa madaraja kadhaa.",
"Pierre, South Dakota\nPierre ndiyo mji mkuu katika jimbo la South Dakota. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2000, mji una wakazi wapatao 14,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 442 kutoka juu ya usawa wa bahari.",
"Umoja, Sudan\nUmoja (\"Kar. الوحدة al-wahda\") ni moja ya majimbo (\"wilayat\") 10 ya Sudan Kusini. Lina ukubwa wa eneo la 22,122 km 2 na wakazi wanaokadiriwa kuwa 4,700,000 (2000). Bentiu ndio mji mkuu wa jimbo hili. Lina wilaya tisa na ni eneo la mafuta baadhi ya mashamba yenye utajiri mkubwa wa mafuta.",
"Columbia, South Carolina\nColumbia ndiyo mji mkuu katika jimbo la South Carolina. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2008, mji una wakazi wapatao 730,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 89 kutoka juu ya usawa wa bahari.",
"Mkoa wa Kusini (Zambia)\nMkoa wa Kusini (\"Southern Province\") ni moja ya mikoa 9 ya kujitawala ya Zambia lenye wakazi 1,212,124 kwenye eneo la 85,283 km². Mji mkuu ni Livingstone.",
"South Carolina\nMji mkuu pia mji mkubwa wa jimbo ni Columbia. Kati ya miji mingine yenye maana ni Charleston, Greenville, Spartanburg, Anderson, Sumter, and Florence.\nSouth Carolina ilikuwa koloni ya Uingereza tangu 1729 na pia moja kati ya koloni 13 zilizoasi dhidi ya Uingereza mwaka 1776 na kuunda nchi mpya ya Marekani tangu 1778.`"
] | 26
|
Akwilina Akwilini Bafta alizaliwa mwaka gani?
|
[
"Akwilina Akwilini\nAkwilina Akwilini Bafta (1 Aprili 1996 - 16 Februari 2018) alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha usafirishaji Dar es Salaam (NIT) ambaye alifariki baada ya kupigwa risasi ya kichwa kimakosa na afisa wa polisi aliyekuwa anajaribu kutuliza ghasia za waandamanaji wa kisiasa wa CHADEMA mnamo tarehe 16 Februari Ijumaa, 2018 huko Kinondoni. Tukio hili la kusikitisha limeamsha hisia kali sana katika mitandao ya kijamii nchini Tanzania. Wengi wamelaani kitendo cha askari kutumia risasi za moto kutuliza ghasia za kisiasa. Tena kwa watu ambao hawana silaha yoyote na wanafanya maandamano ya amani bila fujo. Baada ya tukio, kumekuwa na maswali mengi inawezekana vipi risasi iliyopigwa juu, impige mtu upande wa kushoto ubavuni itokee kulia. Baada ya tukio, polisi sita wahojiwa kuhusiana na tukio hilo la kusikitisha. Siku mbili tangu tukio kutokea, Rais wa Tanzania John Joseph Pombe Magufuli amelaani vikali tukio hilo lisilo la kibinadamu dhidi ya mwanafunzi huyo, na kuwataka wale wote waliohusika wafikishwe katika vyombo vya sheria. Baada ya hili kutokea, ukaanza msako wa kumtafuta mchawi aliyesababisha tukio hili, na hatimaye wakaungukia katika upande wa kisiasa. Hasa akina Mbowe na kikosi chake cha CDM kilichoshutumiwa kwa kufanya maandamano haramu yasiyo na kibali. Hata hivyo, viongozi wa juu wa CDM waliripoti polisi, na hatimaye kuachiwa kwa dhamana huku kukiwa na taarifa ya kwamba uchunguzi haujakamilika na wataitwa tena mara tu uchunguzi dhidi yao utakapokuwa tayari.",
"Akwilina Akwilini\nAkwilina alizaliwa tarehe 1 Aprili, 1996, katika Kijiji cha Marangu Kitowo, Kata ya Olele, wilayani Rombo, Kilimanjaro. Alipata elimu yake ya msingi katika Shule Kitongoria na kuhitimu 2009. Halafu baadaye sekondari alisomea mkoani Iringa na kuhitimu 2014. Baadaye, alichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Embauwai, iliyoko Ngorongoro, Arusha. Kutokana na afya yake kumletea shida akiwa mkoani Arusha, ililazimika kuhama mkoa na kwenda kumalizia elimu ya sekondari kidato cha tano na sita tena mkoani Iringa na kumaliza mwaka 2016. Kuanzia Oktoba 2017, alianza masomo yake katika chuo kikuu cha usafirishaji (NIT) hadi umauti unamfika 16 Februaria, 2018. Hapo NIT alikuwa anachukua shahada ya kwanza ugavi na ununuzi. \nSiku ya Ijumaa mnamo tarehe 16 Februari, 2018 ni siku ambayo CHADEMA na kikosi chake walikuwa wanafanya maandamano ya amani ya kushinikiza kupewa fomu za viapo. Wakati wa maandamano haya, inasemekana polisi walitokea kwa mbele na kutoa onyo za mdomo na kuwataka waandamanaji kusitisha maandamano ambayo hayajapewa kibali. Onyo hizo ziliambatana na maneno makali yaliyokuwa yakisemwa iwapo waposimama hatua kali zitachukuliwa dhidi ya waandamanaji. \nPunde si punde, makabiliano kati ya jeshi la polisi na wafuasi wa chama cha Chadema, yakaanza na kwa maelezo ya jeshi la polisi wanasema walipiga risasi juu ili kutawanyisha waandamanaji na kwa bahati mbaya sana risasi imerudi chini na kumpiga upande wa kushoto Bi. Akwilina Akwilini. Mwanafunzi huyo wa chuo cha usafirishaji Tanzania NIT ambaye baada ya tukio jina lake na picha vilisambazwa katika mitando ya kijamii alipigwa risasi akiwa ndani ya basi au maarufu kama daladala jijini Dar es salaam siku ya Ijumaa majira ya jioni, ikiwa siku moja kabla ya uchaguzi mdogo wa eneo ubunge la kinondoni kufanyika."
] |
[
"Abeti Masikini\nElisabeth Jean Finant (9 Novemba 1954 - 28 Septemba 1994) alikuwa mwanamuziki maarufu wa dansi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Alitambulika sana kwa jina la kisanii kama Abeti Maskini na Afrika Mashariki alijulikana sana kwa kuimba Kiswahili, hasa ule wimbo wake wa \"Likayabu\" (Manjano na amdalasini). Abeti alikuwa chotara kama Jolie Detta, baba yake mzazi akiwa ni mchanganyiko wa Mkongomani na Mbelgiji. \nAbeti alikuwa fundi wa muziki akiwa katika umri mdogo sana ambao hakuna aliyetegemea hasa kwa jinsia yake. Mbali na hapo, alifanikiwa kuwawezesha wasanii waliokuja kuwa wakubwa baadaye, Mbilia Bel na Tshala Muana. Mbilia alikaa katika chungu cha Abeti na kupikwa vilivyo kuanzia kuimba hadi kunengua kuanzia mwaka 1976 hadi 1981. Tshala Muana yeye kuanzia mwaka 1978 hadi 1979. Yondo Sister alipikwa na Abeti katika mwaka 1986. Mwingine ni mwanamama Abby Surya (1984 - 1986).",
"Alice Lakwena\nAlizaliwa kwa jina la Alice Auma. Baada ya ndoa mbili zilizotengwa alikuwa Mkatoliki. Tar. 25 Mei 1985 alishikwa na mapepo akaonekana kama kichaa. Baada ya kupotea kwa siku 40 akarudi kama mganga wa kienyeji akiwa na kipaji cha kuwasiliana na mizimu kufuatana na utamaduni wa Kiacholi.",
"Emmanuel Ake\nWakati Ake alienda nchini Denmark kwa mara ya kwanza mwaka wa 2000, alijitambulisha kama Ali Rajab Akida, au Ali Akida, tu huku akisema kuwa alizaliwa mnamo 20 Desemba 1982. Baadaye ilikuja kugunduliwa kwamba taarifa hii ilikuwa si sahihi na kwamba jina lake halisi lilikuwa Emmanuel Ake Richard Muttendango, aliyezaliwa mnamo 11 Juni 1980. Ake hatimaye alipigwa faini ya DKK(pesa za Denmark) 7,000 na Mahakama ya mji mkuu wa Gladsaxe. Baada ya idadi ya maamuzi na rufaa kutoka pande zote husika, Kamati ya Kitaifa ya Olimpiki na Shirikisho la Michezo la Denmark lilimpiga marufuku kwa muda wa miezi 3. Klabu ya Ake wakati huo, Akademisk Boldklub, pia ilipigwa faini ya 50,000 DKK na alama zote za timu ya kwanza na timu hifadhi za AB zilizokusanywa katika mechi ambazo Ake alishiriki, ziliondolewa.",
"Akwilina Akwilini\nKulingana na mashuhudia, wanasema kuwa maafisa wa polisi walitumia vitoa machozi na risasi katika harakati za kuwatawanya mamia ya wafuasi wa chama cha Chadema waliokuwa wakiandamana hadi afisi za tume ya uchaguzi. Katika mbilinge hilo, baadhi ya wanachama wa CDM walikamatwa. Baada ya taarifa kuenea, shirika la habari la BBC walienda kuzungumza na mkuu wa chuo cha NIT Prof. Zacharia Mganilwa alithibitisha kuwa mwanafunzi wao wa shahada ya Manunuzi na Ugavi Akwilina Akwilini alifariki dunia siku ya Ijumaa. Mganilwa alisema kuwa mwili wa msichana huyo ulikuwa na jeraha la risasi kichwani.\nBaada ya masiku kupita na ndugu wa familia kutaka kujua chanzo cha umauti wa binti yao, ripoti ikaja amepigwa na ncha kali. Majibu ambayo wengi hawakuyapenda. Baada ya joto kuwa kubwa mtandaoni wakihoji uhalali wa majibu mepesi kwa maswali mazito, ndipo jibu lilipotoka ya kwamba chanzo ni risasi iliyopigwa hewani na kupoteza mwelekeo. Taarifa za awali zilikuwa zinasema ya kwamba suala la uchunguzi litachukua takribani siku 14, ndipo walipoazimia kuchukua mwili wa marehemu kwa ajili ya maandalizi ya maziko huku wakisubiri ripoti ya mwisho. Baada ya majadiliano ya ndani ya familia, walikuja na bajeti ya shilingi za Kitanzania milioni themanini lakhi moja na elfu hamsini (80,150,000). Bajeti hii ilizua taharuki kubwa mno mtandaoni. Wengine waliona kama usanii, wengine kufa kufaana, na wengine waliona kama vile kufanya mtaji suala la kuzika.\nMchanganuo wa bajeti wa bajeti hiyo ya familia unaonesha kuwa jeneza ni Sh milioni 1.5, malipo hospitali Sh 200,000, gari ya kusafirisha mwili Sh milioni 3, magari ya kusafirisha wafiwa makubwa matano Sh milioni 20, chakula njiani Sh milioni 3, chakula kwenye msiba Mbezi kwa siku tatu Sh milioni 10, viti 200 Sh 400,000. Turubai kwa siku tatu ni Sh 600,000, mwongoza shughuli Sh 400,000, picha Sh milioni 1 na maji ya kutumia nyumbani Sh 50,000. Kwa pande wa Rombo, Kilimanjaro, chakula kwa siku tano ni Sh milioni 30, muziki na mwongoza shughuli Sh 200,000, turubai Sh milioni 1, viti Sh 400,000, kinywaji cha mabora Sh 100,000, kaburi la kisasa Sh milioni 3, maua na mataji Sh milioni 1, mapambo Sh 500,000 na dharura na tahadhari Sh milioni 2. Awali, ilionekana kama kuna mgomo baridi kutoka serikalini kuhusu kugharamia mazishi hayo kwa bajeti iliyotajwa, lakini baada ya muda kadhaa serikali iliridhia lakini kwa masharti ya kugharamia yenyewe mazishi na si kutoa fedha taslimu. Baada ya mivutano mingi, hatimaye hatua ya maziko ya Akwilina yalianza Dar es Salaam katika viwanja vya chuo NIT tarehe 22 Februari 2018 kumuaga kwa watu wa DAR, halafu tarehe 23 Februari safari ya kwenda Rombo kwa maziko.",
"Édith Piaf\nEdith Piaf (19 Desemba 1915 – 11 Oktoba 1963) alikuwa mwimbaji nchini Ufaransa aliyependwa sana na wananchi.\nJina lake la kuzaliwa ni Edith Giovanna Gassion lakini alichukua jina la kisanii \"Piaf\" (kifaransa kwa ndege shomoro). Wazazi walikuwa wahamiaji kutoka Italia, bibi yake upande wa mama alikuwa berberi kutoka Afrika Kaskazini. Wazazi hawakumtunza walimwachia kwa bibi upande wa baba na huyu alioongoza nyumba ya makahaba mjini Bernay (Normandie). Hapa alitunzwa na makahaba; kuna kumbkumbu ya kwamba alionjeka alipokuwa na miaka 5 akawa kipofu lakini makahaba wote walisimamisha kazi yao kwa siku tatu wakamwombea kanisani akaponyeka.",
"Yosefina Bakhita\nMabwana wapya wa Bakhita walikwenda naye Zianigo, karibu Mirano Veneto, kilometa 25 (maili 16) magharibi kwa Venice. Huko aliishi miaka mitatu akawa yaya wa Alice Michieli, ambaye aliitwa pia \"Mimmina\", na aliyezaliwa mnamo Februari 1886.",
"Violet Barasa\nViolet Awindi Barasa (alizaliwa 21 Juni 1975, katika kijiji cha Sikhendu , Wilaya ya Bungoma, nchini Kenya na alifariki 12 Februari 2007, Webuye) alikuwa mchezaji wa voliboli wa Kenya. Jina lake la kiasili pia huandikwa Baraza .\nAlikuwa nahodha wa muda mrefu wa timu ya wanawake ya kitaifa ya voliboli ya Kenya. Baraza alishiriki akiwa kwenye yimu ya Kenya katika michezo ya olimpiki ya 2000 na 2004 , mara tatu kwenye Kombe la Dunia la Voliboli na kwenye mapambano kadhaa ya bara Afrika. .\nAlikuwa miongono mwa Wakenya wachache kucheza voliboli ya kulipwa katika nchi za ng'ambo, akichezea kilabu cha Al-Ahly nchini Misri, Vileo na Unic-Romania nchini Romania, Panellinios nchini Ugiriki na Chuo Kikuu cha Dicle nchini Uturuki .\nAlifariki mnamo Februari 2007 katika Hospitali ya Wilaya ya Webuye na sababu za kifo chake hazikuwekwa wazi. Wakati wa kifo chake, alikuwa bado mchazaji wa kawaida na kilabu cha voliboli cha Kenya Commercial Bank ,ingawa alikuwa amechujwa kwenye kikosi cha kitaifa.\nAlikuwa ameoleka kwa Kenneth G. Kimani, aliyezaliwa katika kata ndogo ya t Karatun, kata ya Ndarugu ,wilaya ya Kiambu , taarafa ya Gatundu katika Mkoa wa Kati. Alisomea shule ya msingi ya Ndarugu na kisha kijiunga na shule ya upili ya Muhoho, na kisha baadaye kujiunga na Chuo kikuu cha Jomo Kenyatta ,Juja.\nKen kama mkewe, alikuwa miongoni mwa Wakenya wachache kucheza voliboli ya kulipwa katika mataifa ya ng'mbo ,akichezea Panellinios nchini Ugiriki Chuo Kikuu cha Dicle nchini Uturuki .\nKenneth na Awindi hawakuwa na mtoto.\nKen sasa ndiye msimamamizi wa GTN (Gospel Television Network)",
"Amina Chifupa\nAmina Chifupa Mpakanjia alizaliwa tarehe 20 Mei, mwaka 1981 na amefariki tarehe 26 Juni 2007. Mh. Chifupa alisoma shule ya msingi Ushindi na kujiunga na masomo ya sekondari Kisutu kabla ya kuingia shule nyingine ya sekondari ya Makongo alikomaliza elimu ya kidato cha sita mwaka wa 2001."
] | 35
|
Je,Fransisko wa Asizi alizaliwa lini?
|
[
"Fransisko wa Paola\nFransisko alizaliwa kwa muujiza katika mji wa Paola, mkoa wa Calabria, Italia, mwaka 1416. Wazazi wake walikuwa wamefikia uzee bila ya kuweza kuzaa, lakini walimuomba Fransisko wa Asizi na kuweka nadhiri kuwa mtoto wao ataitwa Fransisko. Ndipo walipojaliwa kuzaa.",
"Fransisko wa Asizi\nAlizaliwa mwaka 1181 au 1182 mjini Assisi, Italia; alifariki tarehe 3 Oktoba 1226 karibu na mji ule.",
"Basilika la Mt. Fransisko\nBasilika la Mt. Fransisko huko Assisi, (mkoa wa Umbria, (Italia) ni kanisa kubwa lililojengwa kwa muda mfupi (1228-1253) ili kutunza masalia ya Fransisko wa Asizi (1182-1226)."
] |
[
"Waklara\nBinti huyo wa ukoo bora alizaliwa Asizi (Italia) mwaka 1193. Kisha kuvutiwa na mifano ya Fransisko, na kusikiliza mahubiri na mashauri yake, akaamua kujiweka wakfu kwa Yesu Kristo katika ufukara mkuu. Basi, akatoroka nyumbani usiku (1212) akamuendea Fransisko huko Porsyunkula ambapo alinyolewa naye na kuvikwa kanzu, kamba na shela nyeusi. Kesho yake asubuhi akapelekwa kwa masista Wabenedikto, na baada ya wiki mbili kwenye monasteri yao nyingine, alipofikiwa na mdogo wake (Anyesi wa Asizi) ambaye pia alipaswa kukabili upinzani mkali wa ukoo wao.",
"Fransisko wa Asizi\n1209 Kisha kurudi Asizi wanne wengine wakajiunga nao: hapo wakaamua waende wote Roma ili kupata kibali cha Papa Inosenti III kusudi wawe na hakika ya kuwa maisha yao yanampendeza Mungu, na waeleweke kwa wote kuwa ni Wakatoliki hasa, si wazushi. Baada ya kuvumilia muda fulani wakafaulu kuongea na Papa kwa msaada wa askofu wa Asizi na wa kardinali Yohane wa Mtakatifu Paulo: mara ya kwanza makardinali wengine walibishana na kutaka kupinga ombi hilo; lakini mara ya pili Papa alitoa kwa sauti kibali chake kwa maisha yao ya kitawa na kwa utume wao wa kuhubiri toba. Labda mwaka huohuo Fransisko alianzisha utawa maalumu kwa waamini wanaoishi katika mazingira ya kawaida ya ulimwenguni, waweze kufuata maisha ya Kiinjili kwa ukamilifu mkubwa zaidi.",
"Fransisko wa Asizi\nBaada ya kanuni kuthibitishwa, Fransisko alikwenda Greccio kujitafutia kimya na upweke. Ndipo alipopata wazo la kuadhimisha Noeli kwa namna mpya ili kuitia maanani zaidi. Kwa msaada wa mtawala wa kijiji hicho, kwa ushirikiano wa wananchi na kwa mahudhurio ya ndugu wengi, liliandaliwa pango lenye majani makavu, ng’ombe na punda, halafu ikaadhimishwa Misa ambapo Fransisko, akiwa shemasi, alisoma Injili na kuhubiri kwa utamu mkubwa. Lengo lilikuwa kuwafanya Wakatoliki wote wakumbuke jinsi Mwana wa Mungu alivyojishusha duniani, si tu kwa kujifanya mtu, bali pia kwa namna alivyozaliwa na alivyoishi. Chaguo lake la ufukara lilitegemea ukweli wa maisha ya Yesu kama mtu wa mwisho na mtu wa mateso. Baada ya miezi michache ufuasi huo wa moja kwa moja ukaja kuthibitishwa na madonda matano aliyotiwa juu ya La Verna.",
"Fransisko wa Asizi\nFransisko wa Asizi (kwa Kiitalia Francesco d'Assisi; tangu utotoni jina la ubatizo Giovanni (Battista), yaani Yohane, liliachwa kutumika; pia ubini mwana wa Petro Bernardone ulikuja kuachwa baada ya wao kushindana) alikuwa mtawa, shemasi na mhubiri wa Kanisa Katoliki.",
"Historia ya Kanisa\nFransisko wa Asizi alizaliwa katika familia tajiri akawa kijana aliyependa sana muziki na sherehe. Vitani alifungwa mwaka mmoja akaanza kumtafuta Mungu.",
"Fransisko wa Asizi\nSala nyingine ya pekee aliitunga si kwa Kilatini, bali kwa lugha yake mwenyewe akiweza hivyo kutokeza kwa urahisi mkubwa zaidi yale aliyokuwanayo moyoni. Ni Utenzi wa Viumbe Vyote, shairi la kwanza la Kiitalia, ambalo alilitunga baada ya usiku wa mateso na majaribu ya kukatisha tamaa mnamo Aprili au Mei 1225, ambapo mwishoni aliahidiwa na Mungu uzima wa milele. Katika furaha isiyoelezeka ya kuwa na hakika hiyo akiwa bado duniani, Fransisko alianza kumsifu Mungu kwa viumbe vyake ambavyo yeye kuliko watakatifu wote alijaliwa kuona vinavyohusiana na Muumba. Tusisahau hali ya afya yake wakati huo, ambapo hakuweza kuona kitu wala kuvumilia mwanga, ila alikumbuka kwa shukrani mazuri yote aliyoyaona hasa katika bonde la Spoleto, ambalo alisema hajaona mahali pazuri zaidi.",
"Fransisko wa Asizi\nKlara alizaliwa mwaka 1193 au 1194, hivyo alikuwa na miaka 12-13 Fransisko alipovua utu wa kale mbele ya mji mzima katika uwanda ule ambako iko nyumba ya Klara. Kwa hakika huyo akaendelea kusikia habari mbalimbali juu ya Fransisko: alivyopata wafuasi, mmojawao Rufino binamu wa Klara; alivyokubaliwa na Papa n.k. Hatujui kama ni kwa sababu hizo kwamba alikataa ndoa mbalimbali mpaka akafikia umri wa miaka 18, wala hatujui kama walikutana mara nyingi kwa mashauri ya kiroho. Ila tunajua kwa hakika kuwa baada ya Klara kukimbia nyumbani usiku na kujiunga na jamaa ya ndugu wadogo, akifuatwa na mdogo wake Mt. Agnesi baada ya wiki mbili tu, Fransisko alitimiza wajibu wa kumlisha kiroho kwa mahubiri, mifano na hata maandishi.",
"Fransisko wa Asizi\nElimu yake ilikuwa ya wastani: alijua kidogo Kilatini, Kifaransa, mashairi na Biblia. Malezi yake yalimfanya hodari hasa katika biashara ili aweze kuendesha shughuli zote za baba yake. Na kweli kabla hajaongoka aliiweza sana kazi hiyo. Kama kawaida ya zamani zile, akiwa na umri wa miaka 20 alianza kuhesabiwa mtu mzima na kujihusisha na siasa na vita pia ili kushika nafasi ya juu zaidi kama sharifu. Ndicho kipeo alichojiwekea. Unakumbukwa ukarimu wake kwa maskini, lakini hata ukarimu huo aliuzingatia ili kutimiza wajibu wa ustaarabu kuliko kwa kumpendeza Mungu. Kwa lengo hilohilo la kujitafutia usharifu akawa askari, na akiwa kifungoni Perugia akazidi kuwachangamkia wote, hata sharifu fulani mkorofi. Kuhusu hali iliyotangulia uongofu wake hatujui zaidi, ila mwenyewe aliona kwamba kuishi kwa kufuata mitindo ya ulimwengu kunamchukiza Mungu.",
"Fransisko wa Asizi\n1182 Mtoto Yohane alizaliwa na kubatizwa. Baba yake, Petro wa Bernardone, akirudi toka safarini akamtajia jina la Fransisko, yaani Mfaransa Mdogo. Baada ya hapo mtoto akalelewa katika anasa, ingawa hatujui kama ujanani aliulinda usafi wa moyo au sivyo. Kwa tabia alikuwa na uchangamfu na huruma sana kwa maskini ingawa aliogopa wenye ukoma. Pamoja na adabu njema alipewa pia elimu kidogo kupitia mapadri, halafu akawahi kuanza biashara."
] | 1
|
Je,idadi ya watu nchini Ufaransa ni ngapi?
|
[
"Ufaransa\nEneo lake ni km² 674,843; na idadi ya wakazi ni 63,044,000."
] |
[
"Eneo la ng'ambo la Ufaransa\nMaeneo haya hutofautiana katika hali ya kisheria lakini wakazi wao wote ni raia wa Ufaransa na kila eneo linachagua wabunge wake kwa bunge la Paris. Isipokuwa maeneo yasiyokaliwa na watu hawana mbunge.\nJumuiya hizi zilianzishwa kwa mabadiliko ya katiba ya Ufaransa mwaka 2003. Kila jumuiya imeundwa kwa sheria ya pekee. Ufaransa hutawala au kudai utawala juu ya visiwa vidogovidogo bila wakazi:Visiwa hivi hudaiwa pia na Madagaska na Tromelin inadaiwa na Shelisheli.",
"Wabaski\nWabaski (kwa Kieuskara euskalduna) ni kabila la watu milioni 2-3 wanaoishi hasa Hispania kaskazini, lakini pia Ufaransa kusini-magharibi, mbali ya wengi waliohamia sehemu nyingine za dunia, hasa Amerika.",
"Mkimbizi\nWakazi wenye asili ya Ulaya, \"Pieds-Noirs\" kwa lugha ya Kifaransa, walijumuisha 10.4% ya idadi jumla ya watu wa Aljeria mnamo mwaka wa 1962. Katika miezi michache tu mnamo mwaka wa 1962, 900,000 kati yao walikimbia nchi hiyo, idadi hiyo ikiwa ndiyo idadi kubwa zaidi ya watu kuhamishwa hadi nchini Ulaya tangu Vita Vikuu vya Pili vya Dunia. Msemo uliotumika katika propaganda ya shirika la FLN likitaja jamii ya Pied-noirs ulikuwa \"sanduku au jeneza\" (\"\"La valise ou le cercueil\"\" kwa lugha ya Kifaransa).",
"Ufaransa\nUfaransa ina pia maeneo mengi ya ng'ambo yaliyokuwa makoloni yake zamani lakini kwa sasa ni sehemu rasmi za Jamhuri ya Ufaransa na wakazi wao ni raia wenye haki zote. Kati ya maeneo haya kuna hasa visiwa katika Amerika ya Kaskazini, Amerika ya Kusini, Bahari ya Karibi, Afrika, Bahari Hindi halafu Bahari ya Pasifiki.",
"Manga\nManga kilifunguliwa katika soko la Ulaya katika miaka ya 1970 ambako Italia na Ufaransa yalionyesha anime katika runinga. Sanaa ya Kifaransa imekopa kutoka Ujapani tangu karne ya 19 (Japonisme), Manga umeonyesha umaarufu sana kwa upana wa wasomaji, karibu asilimia 30% ya mauzo ya komiki nchini Ufaransa ni ya manga tangu mwaka wa 2004. Kulingana na Shirika la Biashara inyotendeka nje ya Ujapani, mauzo ya manga yalifika milioni za dola 212.6 ndani ya Ufaransa na Ujerumani pekee mwaka wa 2006.",
"Mapinduzi ya Ufaransa\nWafalme wa nchi jirani waliamua kushambulia Ufaransa na kulipiza kisasi kwa kifo cha mfalme. Katika joto la vita watu wa vikundi vikali vilipata kipaumbele wakaanzisha kipindi cha udikteta chini ya kamati ya bunge lililoongozwa na Robespierre. Watu wengi (16,000-40,000) walishtakiwa kuwa wasaliti wakauawa hadi upinzani ndani ya bunge ulipofaulu kuwakataa viongozi wakali na kuwaua.",
"Mkimbizi\nKulingana na Agence France-Presse, Ujapani iliwakubali watu kumi tu kuingia nchini kama wakimbizi mnamo mwaka wa 2003, idadi ya watu ya chini kabisa nchi hiyo iliyowakubali kuingia nchini tangu mwaka wa 1997 ilipomkubali mtu mmoja pekee. Ijapokuwa iliwanyima hadhi ya ukimbizi, Ujapani iliwakubali watu 16 zaidi mwaka huo ikitumia misingi maalum ya kibinadamu - pia takwimu ya chini kabisa tangu mwaka wa 1997, ambapo iliwakubali watu watatu. Kwa kulinganisha, watu 336 waliomba kupewa hadhi ya ukimbizi nchini Ujapani mwaka huo, takwimu ya juu zaidi katika muda wa miaka miwili. Mashirika mbalimbali ya kimataifa, pamoja na Ubalozi wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, zimeomba nchi ya Ujapani kuwakubali wakimbizi zaidi.",
"Mapinduzi ya Viwandani\nKulingana na Robert Hughes katika kitabu chake \"The Fatal Shore\", idadi ya wakazi wa Uingereza na Wales, ambayo ilikuwa imebaki katika kiwango bila kusonga cha milioni 6 kutoka mwaka wa 1700 hadi mwaka wa 1740, kiliongezeka pakubwa baada ya mwaka wa 1740. Idadi ya watu wa Uingereza ilikuwa imeongezeka kwa zaidi ya mara mbili kutoka milioni 8.3 mnamo mwaka wa 1801 hadi milioni 16.8 mnamo mwaka wa 1851 na, kufikia mwaka wa 1901, ilikuwa imeongezeka karibu mara mbili hadi milioni 30.5. Kadiri hali ya maisha na huduma za kiafya zilivyoboreka wakati wa karne ya 19, ndivyo idadi ya watu nchini Uingereza ilivyoongezeka maradufu kila miaka 50. Idadi ya watu ya Bara Ulaya iliongezeka maradufu wakati wa kipindi cha karne ya 18, kutoka takriban milioni 100 hadi karibu milioni 200, na kuongezeka maradufu tena wakati wa kipindi cha karne ya 19, hadi karibu milioni 400.",
"Kifaransa\nTakwimu kuhusu matumizi ya Kifaransa hutofautiana. Kadirio ndogo lasema kuna watu milioni 87 wanaotumia Kifaransa kama lugha ya kwanza, na tena milioni 100 wanaoitumia kama lugha ya pili. Kadirio kubwa lataja milioni 112,6 wasemaji wa lugha ya kwanza pamoja na milioni 60,6 wenye uwezo wa kutumia Kifaransa karibu kama lugha ya Mama. Halafu hutajwa takriban milioni 100 -110 wanaotumia Kifaransa kikazi, kibiashara au masomoni jumla takriban milioni 300 wasemaji wa Kifaransa duniani.",
"Emmanuel Macron\nEmmanuel Jean-Michel Frédéric Macron (*21 Disemba 1977) ni mwanasiasa nchini Ufaransa aliyezaliwa mjini Amiens. Mwaka 2017 alichaguliwa na wananchi kuwa rais wa taifa. Akiwa na umri wa miaka 39, Macron akawa rais mdogo zaidi katika historia ya Ufaransa"
] | 53
|
Je,Martin Luther alianzisha Uprotestanti mwaka upi?
|
[
"Uprotestanti\nMartin Luther, daktari wa teolojia na padri mtawa, alisema kuwa Kanisa linapaswa kurejea kwenye mizizi yake, na kutoa uzito zaidi kwa yale yaliyoandikwa katika Biblia. Luther alidhani kuwa Kanisa limekwenda mbali na mafundisho ya awali. Alichapisha tasnifu 95 kuhusu njia ya Kanisa Katoliki. Wengine wanasema, alizipigilia kwenye mlango wa kanisa la Wittenberg, lakini wengine wanasema hii si kweli. Tasnifu 95 zilichapishwa mnamo mwaka wa 1516 au 1517. Kwa maneno hayo, yalianza Matengenezo ya Kiprotestanti.",
"Martin Luther\nTarehe 31 Oktoba 1517, alitolea kimaandishi orodha ya \"Hoja 95 dhidi ya rehema\" (kwa Kijerumani: \"95 Thesen wider den Ablass\") za kupinga mafundisho juu ya vyeti hivyo na mengineyo, akakaribisha wataalamu wote kujadiliana naye. Orodha hiyo ilipigwa chapa na kusambazwa kote Ujerumani. Wakristo na mapadri wengi wenye elimu wakaelewa na kukubali hoja zake. Viongozi wa Kanisa wakaona hatari wakajaribu kumtisha anyamaze, lakini alijitetea kwamba hafundishi kinyume cha imani.",
"Historia ya Kanisa\nMwenyewe alitumia kwa nadra neno urekebisho, lakini likaja kuwa jina la kawaida la matukio yale mengi ya miaka 1517 - 1555, yaani kuanzia uenezi wa hoja 95 za Martin Luther hadi amani ya Augsburg. Kati yake mabishano ya Kikanisa yaliyosababishwa na teolojia ya Luther, yalichanganyikana mapema na siasa, uchumi na utamaduni, kutokana na hali halisi ya wakati huo, mbali kuliko mwenyewe alivyofikiri."
] |
[
"Martin Luther\nHivyo Luther alitengwa na Kanisa, lakini wengi walimfuata. Mwaka huohuo Luther aliitwa mbele ya Bunge la Ujerumani ili ajitetee. Ni kwamba sheria za Dola Takatifu la Roma la Kijerumani zilidai mzushi akamatwe au hata auawe. Alipodaiwa na Bunge la Worms akane baadhi ya mafundisho yake, Luther akasimama mbele ya Mfalme mkuu na wakubwa wote akasema: \"Nisipoonyeshwa kwa shuhuda za Biblia, na kwa hoja zinazoeleweka ya kwamba nimekosea, sitakana\". Upande wake Kaisari Karolo V alitoa hotuba muhimu akijitambulisha kama mzao wa vizazi vingi vya watawala walioona daima ni wajibu wao kutetea imani katoliki «ili kuokoa watu» akasema naye ana wajibu huohuo. Alisisitiza kwamba mtawa mmoja anakosea anapodai kupinga Ukristo wa miaka elfu.",
"Martin Luther\nKumbe katika kubishana na Eck, alipotambua kwamba msimamo wa Kanisa ulivyoelezwa na wawakilishi wake unapingana na Biblia alivyoielewa mwenyewe, umoja huo ulivunjika. Ni kwamba Eck alifaulu kumuonyesha mafundisho yake yalivyopinga msimamo wa Kanisa. Ndipo tu Luther alitambua jambo hilo, lakini alidai Mapapa na Mitaguso wamekosea mara nyingi, hivyo yeye anataka kufuata Biblia. Wakatoliki hawakuwa wanapinga nafasi ya kwanza ya Biblia katika imani, bali ufafanuzi wake binafsi. Lakini Luther aliposhindwa kuona msingi wa matamko ya Roma katika Biblia alianza kumfikiria Papa kama Mpingakristo, akaendelea kufundisha. Alipopelekewa barua ya Papa iliyomtishia kumtenga na Kanisa akaichoma moto mbele ya wanafunzi wake. Kwa hiyo tarehe 3 Januari 1521 akatengwa akatangazwa kuwa mzushi.",
"Martin Luther\nNi hapo kwamba upinzani wa Luther dhidi ya mafundisho juu ya rehema ukaenea kupinga yale juu ya mamlaka. Mwanzoni Luther aliona mamlaka ya Biblia, mababu wa Kanisa na mapokeo yake wanaunda umoja. Hata tarehe 13 Oktoba 1518, Luther alitamka rasmi, tena kwa nguvu, kwamba anakubaliana na Kanisa takatifu la Roma, ingawa hawezi kubadili msimamo bila kupata hakika ya kuwa amekosea. Tarehe 22 tena alisisitiza kuwa mafundisho yake hayapingani na ualimu wa Kanisa la Roma.",
"Martin Luther\nHivyo Wakatoliki wanamuangalia Luther tofauti na zamani. Kwa kipindi kirefu cha maisha yake alikuwa Mkristo na padri wa Kanisa Katoliki. Kwa jumla kwa Wakatoliki mafumbo ya imani yana pande mbili ambazo zisitenganishwe hata zikionekana kupingana: kumbe Luther alipenda kusisitiza mmoja na kukanusha mwingine. Hivyo kwa Wakatoliki mara nyingi alichokiri ni sahihi, alichokanusha si sahihi. Jinsi alivyopinga Upapa na sakramenti saba haiwezi kukubaliwa na Wakatoliki, lakini katika mambo kadhaa anaweza kueleweka. Tatizo lenyewe lililokuwa chanzo cha farakano lile, yaani vyeti vya rehema, miaka michache baadaye liliondolewa na Kanisa lenyewe. Mtaalamu mmoja alisema: “Luther asingetengwa na Kanisa Katoliki la leo, wala mwenyewe asingejitenga siku hizi\".",
"Mtaguso wa Trento\nMtu wa kwanza kulilia mtaguso ambao uamue kati yake na papa alikuwa Martin Luther (1517): huko Ujerumani ombi lake liliungwa mkono na wengi, pamoja na Kaisari Karolo V aliyeuona kuwa njia ya kurekebisha Kanisa lakini pia ya kujiimarisha kimamlaka. Ndiyo sababu kuu iliyomfanya Papa Klementi VII (1523-1534), aliyesimama upande wa Ufaransa, kukataa kabisa kuuitisha.",
"Martin Luther\nMiaka iliyofuata teolojia ya Luther ilikua haraka, ikisababisha mabishano mengine. Aliposhambuliwa alijitahidi kutetea msimamo wake na kujipatia watu wa kumuunga mkono dhidi ya waliotaka kumhukumu kuwa mzushi. Mengi yaliandikwa upande wake na dhidi yake, lakini mabishano pekee ya uso kwa uso yalifanyika huko Lipsia mwaka 1519, kati ya Andreas Bodenstein von Karlstadt na Luther upande mmoja, na mjumbe wa Papa, kwa jina Yohane Eck, upande wa pili.",
"Historia ya Kanisa\nMwanzoni walimwona Luther kuwa padri mdogo tu apaswaye kurudishwa kwenye njia iliyo halali. Papa Leo X hakuona umuhimu mkubwa katika habari zake: mwaka 1521 akamtenga Luther katika Kanisa, halafu akapokea habari za Bunge la Ujerumani lililomhukumu Luther kuwa mzushi na adui wa taifa.",
"Uprotestanti\nLakini watawala waliomuunga mkono Luther walitoa hati ya pamoja inayoanza na maneno \"Protestamur\", yaani \"Tunapinga\".",
"Uprotestanti\nUprotestanti ni aina ya Ukristo iliyotokana na Kanisa Katoliki huko Ulaya Kaskazini katika karne XVI kufuatana na tapo la kidini na la kisiasa maarufu kwa jina la \"Matengenezo ya Kiprotestanti\". Wahusika wakuu wa tapo hilo ni Martin Luther na Yohane Kalvini."
] | 21
|
Je,Mlima kilimanjaro ina urefu wa kilomita ngapi?
|
[
"Kilimanjaro (Volkeno)\nKilimanjaro ni mlima mrefu kuliko yote barani Afrika. Mlima huu uko nchini Tanzania katika Mkoa wa Kilimanjaro. Una urefu wa mita 5,895 (futi 19,340)."
] |
[
"Chile\nChile ina urefu wa kilomita 4,200 kufuata pwani ya Pasifiki na milima ya Andes. Umbali huu ni kama kutoka Cape Town kwenda Dar es Salaam. Lakini upana wa wastani wa eneo lake ni kilomita 180 tu: sehemu nyembamba ya nchi ina upana wa kilomita 90, sehemu pana zaidi ina kilomita 240.",
"Jiografia ya Kenya\nEneo hili la milima ndilo la juu zaidi nchini Kenya (na la pili kwa urefu barani Afrika): Mlima Kenya, unaofikia urefu wa mita 5,199 (futi 17,0570) na ni eneo lenye mito ya barafu. Ng'ambo ya mpaka wa Tanzania Mlima Kilimanjaro () huweza kuonekana upande wa kusini.",
"Kenya\nEneo hili la milima ndilo la juu zaidi nchini Kenya (na la pili kwa urefu barani Afrika): Mlima Kenya, unaofikia urefu wa mita 5,199 (futi 17,0570) na ni eneo lenye mito ya barafu. Mlima Kilimanjaro () huweza kuonekana upande wa kusini, ng'ambo ya mpaka wa Kenya na Tanzania .",
"Dunia\nLakini si tufe kamili. Ina uvimbe kidogo kwenye sehemu ya ikweta; ilhali umbali kati ya ncha mbili ni kilomita 12,713 lakini umbali kati ya sehemu za kinyume kwenye ikweta ni km 12,756, yaani kipenyo hiki kinazidi takriban kilomita 43 kipenyo kati ya ncha na ncha. Tofauti hii inasababishwa na mzunguko wa dunia. Kani nje inasukuma sehemu za ikweta nje zaidi. Kwa hiyo mahali duniani palipo karibu zaidi na anga la nje si Mlima Everest kwenye Himalaya bali mlima Chimborazo nchini Ekuador.\nKwenye uso wake dunia huwa na tofauti kati ya nusutufe zake mbili. Nusu moja ina eneo kubwa la mabara yaani nchi kavu ambayo ni asilimia 47 ya sehemu hii. Kinyume nusutufe nyingine inafunikwa na maji ya bahari na eneo la nchi kavu ni asilimia 11 pekee za maeneo yake.",
"Mlima Longonot\nKilele cha Mlima Longonot una kasoko yenye kipenyo cha kilomita 1.8 na urefu wa mita 200 au zaidi kwenda chini kutegemeana na urefu wa kuta za kasoko. Njia nyembamba inaelekea kutoka kiingilio cha mbuga hadi mdomo wa volkeno, na kuendelea kwenye kona ya kasoko ya volkeno. Ziara nzima ni kilomita 8-9 tu lakini ina mwinuko sana, hivi kwamba safari ya kutoka lango la Hifadhi hadi kilele cha Longonot na kurudi tena langoni huchukua takriban masaa 5 kwa miguu. Lango liko aghalabu mita 2150 juu ya usawa wa bahari na upeo unafikia mita 2760 m juu ya usawa wa bahari lakini kufuatia mzunguko wake usio sawa kunahusisha zaidi ya tofauti ya mita 630.",
"Mweru (ziwa)\nUrefu wa ziwa ni kilomita 118 na upana wake km 45 likielekea kutoka kaskazini mashariki kwenda kusini magharibi. Uso wa ziwa uko mita 917 juu ya UB kwa hiyo uko juu kuliko Ziwa Tanganyika kwa m 763. Ni moja ya maziwa ya bonde la ufa likiwa katika mkono wa pembeni wa Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki. Mwambao wa magharibi ni mtelemko mkali jinsi ilivyo mara nyingi kwenye maziwa ya bonde la ufa unaopaa hadi milima ya Kundelungu.",
"Olympus Mons\nOlympus Mons ina urefu wa kilomita 27 juu ya uso wa Mirihi wastani. Hivyo kimo chake ni mara tatu kuliko Mlima Everest duniani ukipimwa kutoka usawa wa bahari na zaidi ya mara mbili kuliko Mauna Kea unaopimwa kilomita 10 kutoka mguu wake chini ya bahari hadi kilele.",
"Milima ya Maji Moto\nKilele kina urefu wa mita 1,257 juu ya usawa wa bahari.",
"Masai Mara\nHifadhi Mbuga ya Wanyamapori ya Kitaifa ya Masai Mara ina upana wa kilomita 1530 kieneo upande wa Kusini Magharibi mwa Kenya. Ndiyo sehemu ya Serengeti iliyo upande wa Kaskazini zaidi yenye upana wa jumla ya kilomita 25,000 kilomita kieneo. Upande wa Kusini imepakana na muga ya wanyama ya Serengeti, na upande wa magharibi na mharara wa Siria na upande wa Kaskazini Mashariki na Magharibi imepakana na maeneo ya ufugaji. Kiwango cha mvua katika mazingira haya huongezeka kuanzia kusini-mashariki-hadi magharibi, japo hubadilika kiwakati kutoka eneo moja hadi lingine na ni ya misimu miwili. Mito ya Sand, Talek na Mara ndiyo mito mikubwa ambayo hutoa maji kwenye hifadhi ya mbuga hii. Vichaka na miti iliyomea kwenye kingo za mito hufunika miteremko na vilele vya milima\nKimsingi mandhari ya hifadhi hii ni nyasi iliyowazi na mito. Eneo la Kusini Magharibi kuna vichka vya aina mbalimbli ya miti ya aina ya mwangate. Upande wa mpaka wa magharibi kuna harara(genge) la Esoit Oloololo la Bonde la Ufa, na wanyamapori wanapatikana eneo hili kwa wingi kwa sababu chemichemi ya maji hupatikana kwa urahisi na hakuna usumbufu wa watalii. Mwisho wa mpaka wa Mashariki ni kilomita 224 kutoka Nairobi, kwa hivyo, ni upande wa mashariki ndio hutembelewa na watalii sana.",
"Milima ya Mugongo\nKilele kina urefu wa mita 1,325 juu ya usawa wa bahari."
] | 48
|
Maktoum bin Rashid Al Maktoum alikuwa makamu wa rais wa falme ipi?
|
[
"Maktoum bin Rashid Al Maktoum\nSheikh Maktoum bin Rashid Al Maktoum alifariki asubuhi ya 4 Januari 2006, baada ya 'heart attack' kama amekaa katika hoteli ya Palazzo Versace iliyo katika Gold Coast, Queensland, Australia. Nafasi yake ilichukuliwa na ndugu yake, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum kama mtawala wa Dubai.",
"Mohammed bin Rashid Al Maktoum\nBaada ya muongo wa utawala usio na ubishi,[4] ^ Ripoti ya BBC, 2006/01/05 yeye akawa mtawala wa Dubai tarehe 4 Januari 2006 baada ya kifo cha ndugu yake Sheikh Maktoum bin Rashid Al Maktoum. Pia aliteuliwa na Rais wa UAE, Sheikh Khalifa bin Zayed Al Nahyan, kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa UAE tarehe 5 Januari 2006. Wajumbe wa Baraza la Taifa la Shirikisho la UAE waliyakubali mapendekezo ya Rais muda mfupi baadaye.",
"Maktoum bin Rashid Al Maktoum\nMaktoum bin Rashid Al Maktoum (1943 - 4 Januari 2006) (Kiarabu: مكتوم بن راشد آل مكتوم) pia anajulikana kama Sheikh Maktoum (la heshima) alikuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Emir au mtawala wa Dubai.",
"Mohammed bin Rashid Al Maktoum\nTarehe 3 Januari 1995, Sheikh Maktoum bin Rashid Al Maktoum alisaini amri mbili ambazo zilimteua Sheikh Mohammed kama Mkuu Mteule wa Dubai.",
"Mohammed bin Rashid Al Maktoum\nMohammed bin Rashid Al Maktoum (Kiarabu: محمد بن راشد آل مكتوم; pia Sheikh Mohammed , (aliyezaliwa 15 Julai 1949), ni Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE), na Emir wa Dubai."
] |
[
"Rashid Bin Saeed Al Maktoum\nAliyemtangulia (kama Waziri Mkuu) na mrithi wake alikuwa mwana wake, Sheikh Maktoum bin Rashid Al Maktoum, ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa United Arab Emirates 1971-1979 na ambaye alikuwa Emir ya Dubai kuanzia 7 Oktoba 1990 hadi kifo chake tarehe 4 Januari 2006. Mwanake mwengine, Mohammed bin Rashid Al Maktoum, alichukua nyadhifa hizi zote baada ya kifo cha Sheikh Maktoum.\nMmoja wa viongozi wenye mafanikio zaidi katika Mashariki ya Kati, Sheikh Rashid aliwajibika kwa ajili ya mageuzi ya Dubai katika mji wa bandari ya kisasa na kibiashara. Laini yake maarufu, \"\"babu yangu aliendesha ngamia, baba yangu aliendesha ngamia, mimi naendesha Mercedes, mwanangu aendesha Land Rover, mwanake ataendesha Land Rover, lakini mwanake ataendesha ngamia.\"\" Huangazia wasiwasi wake kwamba mafuta ya Dubai yataisha katika muongo mmoja au mbili. Hivyo alifanya kazi ili kujenga uchumi katika Dubai ambao unaweza kuishi baada ya mafuta ya Dubai kuisha.",
"Rashid Bin Saeed Al Maktoum\nSheikh Rashid Bin Saeed Al Maktoum (1912 - 7 Oktoba 1990) (Kiarabu: راشد بن سعيد آل مكتوم) alikuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu na Emir (mtawala) wa Dubai. Yeye alitawala kwa miaka 32, mpaka kifo chake.\nSheikh Rashid Bin Saeed Al Maktoum anaweza kuitwa aliyekuwa na maona ya UAE ya kisasa Ilikuwa wakati wa utawala wake ambapo Dubai ilikua kutoka mji mdogo wa kibiashara hadi mji mkuu wa mkusanyiko. Kufuatia uvumbuzi wa mafuta katika kanda hiyo katika miaka ya 1960, moja ya majukumu yake ya kwanza ilikuwa ni ya ujenzi wa bandari ya kisasa na viwanja vya ndege Dubai. UAE ilishuhudia shughuli nyingi za ujenzi katika miaka ya 1970 na nyingi zilikuwa zikifanyika Dubai. Ujenzi wa bandari ya pili katika Jebel Ali, Dubai Dry Dock, Shindaga Tunnel na Dubai Trade Center kwa kutaja wachache. Miradi hizi zimefungua njia ya maendeleo ya baadaye ya mji ambayo yanaendelea mpaka leo. Bintiye aliolewa na kisha Emir wa Qatar ambaye alisaidia katika kugharimia miradi zingine. Emir wa Kuwait alisaidia katika ufadhili wa uchimbaji wa Creek, ambayo ilisababisha Dubai ifanikiwe kama bandari ya kuingia UAE. Mama yake Sheikha Hussah bint Murr alimiliki ardhi, alihusika katika biashara na aligawana uongozi wa Dubai.\nSheikh Rashid alikuwa na wana wanne:",
"Maktoum bin Rashid Al Maktoum\nMzaliwa wa Al Shindagha, Dubai kwa familia ya Al Maktoum, kabila ya Al Bu Falasah, alikuwa Waziri Mkuu mara ya kwanza tarehe 9 Desemba 1971 na kutumikia hadi 25 Aprili 1979 wakati nafasi yake ilichukuliwa na baba yake, Sheikh Rashid Bin Saeed Al Maktoum. Kufuatia kifo cha babake 7 Oktoba 1990 aliichukua nafasi yake kama Waziri Mkuu na kama mtawala wa Dubai. Alitumikia katika nyadhifa zote mbili hadi kifo chake tarehe 4 Januari 2006.",
"Mohammed bin Rashid Al Maktoum\nSheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum amejulikana kwa michango yake mikubwa Tarehe 19 Mei 2007, alitangaza mipango ya kutoa $ 10bn dola na kuanzisha shirika la usaidiza la Mohammed bin Rashid Al Maktoum, shirika la usaidizi la elimu katika Mashariki ya Kati, moja ya michango ya hisani kubwa zaidi katika historia. Sheikh Mohammed alisema kuwa fedha hizo ni za kuweka daraja la kuziba pengo la maarifa kati ya Uarabuni na Kanda zilizoendelea, kuboresha kiwango cha elimu na utafiti katika kanda, kuendeleza mipango ya uongozi kwa vijana, na kuchochea ajira. Tangazo hili lilifanywa mwaka 2007 katika World Economic Forum nchini Jordan. Jumla ya thamani yake halisi kwa sasa, Hata hivyo, inasemekana kuwa tu $ 16bn.",
"Maktoum bin Rashid Al Maktoum\nSheikh Maktoum pia aliwahi kuwa Rais wa Falme za Kiarabu tarehe 2-3 Novemba 2004 kufuatia kifo cha Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan mpaka Sheikh Khalifa bin Zayed Al Nahyan alipotangazwa kama Rais wa Muungano wa Falme za Kiarabu tarehe 4 Novemba 2004."
] | 43
|
Idadi ya watu wa Nchini Meksiko ni ngapi?
|
[
"Mexiko\nWakazi ni 118,395,054: wengi wao ni machotara wenye damu ya Wahindi wekundu (31/55% hivi) na Wazungu (42/65% hivi). Wenye asili ya Ulaya tu ni 9/18%."
] |
[
"Texas\nTexas ni jimbo la kujitawala la Maungano ya Madola ya Amerika au Marekani. Idadi ya wakazi wa jimbo lote hufikia watu 24,326,974 (2008) wanaokalia eneo la 696,241 km² ambalo ni hasa milima na jangwa. Upande wa mashariki ni maji ya ghuba ya Meksiko. Mji mkuu wa jimbo ni Austin na mji mukubwa jimboni ni Houston. Imepakana na Oklahoma, Arkansas, Louisiana, New Mexico (Meksiko Mpya) na nchi ya Meksiko (Chihuahua, Coahuila, Nuevo León na Tamaulipas).",
"Kisiwa cha Migingo\nKisiwa kina wakazi wapatao 250 (makadirio yanatofautiana), hasa wavuvi na wafanyabiashara wa samaki, ambao hutumikiwa na vilabu, idadi ya madanguro na duka la madawa katika kisiwa hicho.\nKipande cha ardhi kilicho na mawe na mimea kidogo, Migingo ni mojawapo ya visiwa vitatu vidogo inayokaribiana. Kama ilivyo wazi katika Google Earth, kisiwa cha Usingo kilichokuwa kikubwa zaidi kiko mashariki mwa \"kitone\" kidogo cheupe yaani Migingo, na Kisiwa cha Piramidi, kubwa zaidi ya hivi vitatu, kiko kusini mwa Migingo na kaskazini mpakani mwa Tanzania katika Ziwa Victoria. Katika ramani, visiwa vyote vitatu vimekuwa vikionyeshwa kuwa upande wa Kenya kutoka mwaka wa 1920, wakati \"Kenya Colony and Protectorate Order in Council, 1926\" lilitoa tuzo la visiwa vyote vitatu nchini Kenya.\nMigingo ni kisiwa kidogo hadi haijaonyeshwa katika baadhi ya ramani. Hata hivyo, haija \"ibuka kutoka majini\" hivi majuzi, licha ya madai rasmi ya serikali ya Uganda. Katika muongo wa kwanza wa karne ya 21, maji yameshuka 0.5-1.0 mita tu (futi 1-3) katika ziwa kutoka ngazi ya kawaida.",
"Kata ya Antelope, Nebraska\nKatika sensa ya mwaka wa 2000, kulikuwa na watu 7452, kaya 2953 , familia 2073 zilizoishi katika kata hii. Wiani ya wakazi ilikuwa watu 9 katika maili 1 mraba (3/km ²). Kulikuwa na vitengo vya nyumba 3,346 katika wiani ya wastani ya 4 kwa kila maili mraba (2/km ²). Ujumuisha awa rangi ulikuwa 98.82% weupe, 0.05% weusi au Afrika Amerika, 0.31% Amerika wa Asili, 0.05% Asia, 0.28% kutoka jamii nyingine, na 0.48% kutoka jamii mbili au zaidi. 0.70% ya idadi ya watu walikuwa wahispani au Latino wa rangi yoyote. 57.9% walikuwa wa Kijerumani, 6,6% Waingereza , 6,6% Amerika na 5,9% asili ya Kiayalandi kulingana na Sensa ya 2000.\nKulikuwa na kaya 3640 ambazo 36.0% zilikuwa na watoto chini ya umri wa miaka 18 , 62.50% walikuwa wamefunga ndoa , 5.50%zilikuwa na mwanamke bila bwana , na 29.80%zisizo na familia. 26.3% ya kaya zote ni watu binafsi na 16.20%ni mtu anayeishi peke yake ambaye alikuwa na umri wa miaka 65 au zaidi. Ukubwa wa wastani wa kaya ulikuwa 2.49 na ukubwa wa familia ya wastani ilikuwa 3.05. .\nKatika kata hii wakazi walitandaa kote kwa 27.50% chini ya umri wa miaka 18, 6.20% 18-24, 23.30% 25-44, 23.20% 45-64, na 19.90% ambao walikuwa na umri wa miaka 65 au zaidi. Umri wa wastani ulikuwa miaka 31. Kwa kila wanawake 100 kulikuwa wanaume 96.80 Kwa kila wanawake 100 katika umri wa 18 na juu, kulikuwa na wanaume 94.30.\nMapato ya wastani kwa kaya katika kata hii ilikuwa $ 30.114, na kipato cha wastani kwa familia kilikuwa $ 36.240. Wanaume walikuwa na kipato cha wastani cha $ 26.288 dhidi ya $ 16.926 kwa wasichana. Pato la wastani la kata hii lilikuwa $ 14.601. Karibu 10.30% ya familia na 13.60% ya idadi ya watu walikuwa chini ya mstari wa umaskini, ikiwa ni pamoja na 17.20% ya wale walio chini ya umri wa 18 na 11.90% ya wale walio na wa 65 au zaidi.",
"Honduras\nWakazi walio wengi kabisa (90%) ni machotara hasa wenye asili ya mchanganyiko wa Waindio na Wazungu. Hao ndio asilimia 90 ya wakazi wote. Katika misitu ya milimani kuna bado vikundi vya wenyeji asilia (Wahindi wekundu, 7%). Wengine ni wa asili ya Afrika (2%) au ya Ulaya (1%) wasiochanganyika sana na wengine. Kwenye pwani ya kaskazini kuna makazi ya Wagarifuna ambao wana utamaduni wa mchanganyiko wa Wahindi wekundu na Waafrika.",
"Arizona\nArizona ni jimbo la kujitawala la Maungano ya Madola ya Amerika au Marekani. Idadi ya wakazi wa jimbo lote hufikia watu 6,500,180 (2006) wanaokalia eneo la 295,254 km² ambalo sehemu kubwa ni milima na jangwa. Mji mkuu na mji mukubwa jimboni ni Phoenix. Imepakana na Utah, New Mexico (Meksiko Mpya), Mexiko (Sonora na Baja California), California na Nevada. Kuna lugha rasmi 3: Kiingereza (74.1%), Kihispania (19.5%) na Kinavaho (1.9%).\nState of Arizona Official Website",
"New Mexico\nMji mkuu wa jimbo ni Santa Fe. Mji mkubwa ni Albuquerque. Idadi ya wakzi wa jombo lote hufikia watu 1,819,046 wanaokalia eneo la 315,194 km² ambalo ni hasa milima na jangwa.",
"Martinique\nIdadi ya wakazi ni 386,486. Takriban 90% ni wa asili ya Afrika au machotara wa aina mbalimbali. Wazee wao waliletwa huko kama watumwa kwa ajili ya kazi katika mashamba ya miwa. Kikundi kikubwa cha pili ni Wazungu (5%). Waliobaki ni Wahindi, Waarabu na Wachina.",
"Nanyuki\nMsingi wake umewekwa mwaka 1907 na walowezi Waingereza, ambao dhuria wao bado wanaishi mjini na katika mazingira yake. Sasa Nanyuki ni kituo kuu cha Jeshi la Anga la Kenya. Jeshi la Uingereza linatunza kituo pia na linaendesha mazoezi kila mwaka mlimani na kwa maeneo kame kaskazini. Nanyuki ni katika kaunti ya Laikipia. \nNanyuki ilikuwa na idadi ya watu ya 49,233 mwaka 2009 (). Wakazi wengi huchuma fedha yao kwa kufanya biashara. Maduka mjini hugawia mashamba, ranchi na hifadhi za wanyama katika mazingira mapana. Kwanza maduka mengi yalimilikiwa na Wahindi ambao bado ni kipande kikubwa kiasi cha wakazi. Wakwezi na wabebashanta hutembelea Nanyuki wakienda na kutoka Mlima Kenya kwa njia za Sirimon na Burguret, na watalii wengi wengine hupitia mji. Kwa hiyo Nanyuki una hoteli nyingi ambazo mwongoni mwao kuna Mount Kenya Safari Club, \"Sportsman’s Arms Hotel\", \"Lion’s Court\", \"Equatorial Hotel\", \"Mount Kenya Paradise Hotel\" na \"Joskaki Hotel\". Mgahawa wa zamani sana ni \"Marina\" ambao bado unapendwa kiasi. Miaka kadhaa iliyopita mgahawa mwingine umefunguliwa kusini kwa Nanyuki ambao umejengwa ndani ya mti mkubwa sana. Unaitwa \"Trout Tree Restaurant\" na mvuto mkuu wake ni trauti apikwaye kwa namna mbalimbali. Wateja wanaweza kutembelea pia msimiko wa kufuga trauti chini ya mti.",
"Niger\nMipaka ilichorwa wakati wa ukoloni wa Ufaransa, ikiunganisha watu wenye utamaduni tofautitofauti, kama vile Watuareg (10.4% za wakazi wote) wa Sahara, wahamaji Wafula (9.9%) na Wakanuri (4.4%) wa eneo la Sahel na wakulima wa kusini kama Wasonghai (21.2%) na Wahausa: hawa wa mwisho ni 53% .",
"Manihi\nManihi ni kisiwa cha Polinesia ya Kifaransa ndani ya funguvisiwa ya Tuamotu. Kiko upande wa magharibi wa kisiwa cha Takaroa. Eneo la kisiwa ni 13 km². Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Paeua. Mwaka wa 2012, idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa 685. Watu wakaao kisiwani kwa Manihi huongea Kituamotu na Kitahiti."
] | 7
|
Kipima joto kiligunduliwa na nani?
|
[
"Kipimajoto\nUgunduzi wa kipimajoto umechangiwa na Galileo, ingawa aina ya kipimajoto kilichozibwa hakikuwepo mpaka mwaka 1650. Vipimajoto vya kisasa vinavyotumia spiriti na zebaki viliundwa na mjerumani Gabriel Fahrenheit ambaye pia alipendekeza kipimio cha jotoridi, kilichoitwa kwa jina lake - Fahrenheit, ambapo 32 F ni jotoridi la kuganda kwa maji na 212 F ni jotoridi la kuchemka kwa maji katika mkandamizo wa hewa wa kawaida. Vipimio vingi vilipendekezwa tangu muda wake. Katika kipimio cha centigrade au celsius, kilichobuniwa na mnajimu wa kiswideni Anders Celsius, ndicho kinachotumika sana dunia. Katika kipimio hiki maji huganda katika 0 C na huchemka katika 100 C."
] |
[
"Nta ya sikio\nWagonjwa mara nyingi wanapenda mchanganyiko wa kumwagilia upashwe joto mpaka kufikia lile joto la mwili.kizunguzungu ni tatizo kuu la unyonyaji kwa kutumia vimiminika ambavyo ni vya baridi au vya joto kuliko joto la mwili. Sharp et al. Alipendekeza 37°C, naye Blake et al. alipendekeza maji yawe 38°C, zaidi kuliko joto la mwili, na kwamba hii lazima ichunguzwe na kipima joto. Joto jingine yoyote inaweza kusababisha kisulisuli, kama hutumika wakati wa upimaji wa jaribio la kalori tendohiari.",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nOngezeko la joto lina matokeo mawili kwa idadi ya vifo ya moja kwa moja ambayo hutendeka kinyume: Idadi kubwa ya vipimo vya joto wakati wa majira ya baridi hupunguza vifo kutokana na baridi; vipimo vya joto vya juu zaidi wakati wa majira ya kiangazi huongeza vifo kutokana na joto. Athari ya jumla ya matokeo haya ya moja kwa moja inatagemea inategemea hali ya anga ya eneo fulani. Palutikof \"na wengineo.\" (1996) alifanya hesabu na kupata kuwa nchini Uingereza na Wales kwa kila ongezeko la 1 °C la kipimo cha joto kupungua kwa vifo kutokana na baridi kunazidi ongezeko la joto kutokana na joto, hivyo basi kusababisha kupungua kwa idadi ya wastani ya vifo ambayo ni 7000, huko Keatinge \"na wengineo.\" (2000) “akidokeza kuwa ongezeko lolote la vifo kutokana na ongezeko la vipimo vya joto huenda likapitwa ndogo likilinganishwa na idadi kupungwa kwa idadi kubwa ya vifo kutokana na baridi.” Cold-related deaths are far more numerous than heat-related deaths in the United States, Europe, and almost all countries outside the tropics. Katika kipindi cha miaka ya 1979–1999, jumla ya vifo 3,829 nchini Marekani vilihusishwa na joto jingi kutokana na hali ya hewa, katika kipindi hicho pia jumla ya vifo 13,970 vilisababishwa miili ya waathirika kupigwa na baridi kali. Barani Ulaya, vifo vya wastani kutokana na joto ni 304 katika eneo la Kasakzini mwa Finland, 445 mjini Athens na 40 mjini London, huku vifo kutokana na baridi vikiwa 2457, 2533, na 3129 mtawalia. Kulingana na Keatinge \"na wengineo.\" (2000), “wakazi Barani Ulaya wamezoea vipimo vya joto vya majira ya kiangazi vya kati ya 13.5°C hadi 24.1°C, na wanatarajiwa kuzoea ongezeko la joto lililotabriwa katika nusu karne ijayo wakiwa na ongezeko ndogo endelevu la vifo kutokana na joto.”",
"Kisima\nViwango vya joto katika kisima vinaweza kutumika kama mibadala ya joto. Hii ni kwa sababu uhamishaji wa joto kupitia ardhini hufanyika polepole, hivyo kwa kupima joto (na kutumia mifumo ya hisabati) viwango vya joto vya zamani vinaweza kurejelewa miaka mia kadhaa mbeleni (Huang et al. 2000) \nKisima cha uyeyukaji wa barafu hakina maji machafu kama ilivyo lkatika visiwa vya mawe. Kisima cha Central Greenland huonyesha : \" joto zaidi ya miaka 150 iliyopita ya wastani wa 1 ° C ± 0.2 ° C iliitangulia na karne chache zenye baridi. ililotangulia hii ilikuwa kipindi cha joto katika AD 1000, ambacho kilikuwa na joto kuliko karne ya 20 kwa wa 1 ° C. \"",
"Kimondo\nKikikaribia mno dunia yetu kinaingia katika angahewa na kuanguka chini kwa kasi kubwa sana. Njiani kinapashwa moto kutokana na msuguano wa hewa dhidi yake. Kiasi cha joto kinatosha kuchoma kimondo kidogo kabisa hewani. Hii inaonekana kwa macho matupu kama mstari wa moto angani unaowaka kwa sekunde 1-2. Hii ni hali inayoitwa pia \"meteori\". Waswahili wa Kale waliita \"Vinga vya sheitani\" walieleza miale hii ya moto angani kuwa malaika angani wanazuia masheitani kupanda juu kwa kuwarushia vipande vya kuni vya kuwaka",
"Kipimajoto\nKipimajoto chochote kile huwa kinapima jotoridi lake chenyewe, ambalo linaweza lisiwiane na jotoridi hasa la kitu linalopima. Katika kupima jotoridi la hewa nje ya jengo, kwa mfano, kama kipimajoto moja itawekwa kivulini na nyingine katika jua, kwa tofauti ya sentimita chache, majibu ya vipimojoto hivi yanaweza kuwa tofauti sana, ingawa jotoridi la hewa sawa. Kipimajoto katika kivuli kinaweza kupoteza joto kwa mnururisho kwa kuta za jengo na hivyo vipimo vikawa vidogo chini ya jotoridi halisi la hewa. Kwa upande mwingie kipimajoto kilichokatika jua kitasharabu joto la jua na kuonyesha kiwango kikubwa kuliko kile halisi cha hewa. Ili kuondoa makosa kama haya, upimaji sahihi wa jotoridi huitaji ukingaji wa kipimajoto kutoka katika vyanzo vya joto au baridi au kutoka joto linaloweza kusafiri kwa mnururisho, mpitisho au myuko.",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nKatika kipindi cha miaka mia hivi kilichopita, rekodi ya joto imeonyesha mwelekeo wa hali ya anga ambapo kipimo cha joto kimepanda, yaani, ongezeko la joto Duniani. Mabadiliko mengine ambayo yameonekana ni pamoja na kupunguka kwa eneo la Aktiki, Kutolewa kwa gesi ya metheni katika eneo la Aktiki, kutolewa kwa gesi ya Kaboni iliyo ardhini katika maeneo yenye mchanga uliofanywa kuwa kama barafu na Kutolewa kwa gesi ya metheni katika madongedonge ya pwani, na kupanda kwa uwiano wa bahari.\nKipimo cha joto cha wastani duniani kinatabiriwa kupanda, pamoja na uwezekano wa visa vya matukio mabaya ya hali ya hewa, na mabadiliko ya ruwaza za mvua. Tukisonga kutoka hali ya maeneo makubwa Duniani hadi hali ya maeneo madogo, kuna ongezeko la uhakika kuhusu jinsi hali ya hewa itakavyobadilika. Uwezekano wa ongezeko la joto kuwa na matokeo ambayo hayakuwa yametarajiwa awali, unaongezeka na kiwango, ukubwa na muda wa mabadiliko ya hali ya hewa. Some of the physical impacts of climate change are irreversible at continental and global scales. Eneo la bahari lenye maji linatarajiwa kupanda hadi kati ya sentimita 18 na 59 (inchi 7.1 hadi 23.2) kufikia mwwisho wa karne ya 21. Kwa sababu ya ukosefu wa maarifa ya kutosha ya kisayansi, makisio haya ya kupanda huku kwa kiwango cha bahari chenye maji hayajumuishi mchango utakaofanywa na mabati ya barafu. Kupunguka kwa Slowing of the Mzunguko wa Kimeridia wa Kupinduka una uwezekano mkubwa wa kufanyika katika karne hii, lakini vipimo vya joto katika eneo la Atlantiki na Ulaya huenda vikawa vikubwa zaidi kwa sababu ya ongezeko la joto duniani. Kwa joto duniani kuongezeka kwa kiwango cha 1-4°C (ikilinganisha kipindi cha kati ya mwaka wa 1990 hadi mwaka wa 2000), kuna uwezekano wa wastani kwamba kuyeyuka kwa sehemu kwa Bati la barafu la Greenland kutatendeka kwa kipindi cha karne nyingi na milenia. Ikihusisha uwezekano wa mchango wa kuyeyushwa kwa sehemu ya Bati la barafu la eneo la Magharibi mwa Antaktiki, eneo lenye maji baharini litapanda kwa kiwango cha kati ya mita 4 na 6 au zaidi.",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nKuongezeka kwa joto huenda kukaongeza kiasi cha usimbishaji Lakini haijulikani kwa kweli jinsi ongezeko la joto litakavyoathiri dhoruba. Dhoruba zinazopatikana nje ya maeneo ya Kitropiki hutegemea gredienti ya kipimo cha joto, ambacho kinatabiriwa kuwa dhaifu kuzidi katika Ulimwengu wa kaskazini huku kanda la ncha ya eneo la kaskazini mwa Ulimwengu likizidi kuwa na joto jingi kuliko maeneo mengine katika ulimwengu wa kasakazini.",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nOngezeko la joto Duniani ambalo halidhibitiwi linaweza kuathiri maeneo mengi ya kiikolojia ardhini. Ongezeko la kipimo cha joto Duniani kunamaanisha ya kuwa mifumo ya kiikolojia itabadilika; baadhi ya spishi wanalazimishwa kuhama makazi yao (huku viumbe hao wakikabiliana na uwezekano wa kuangamia) kwa sababu ya hali ya anga inayobadilika, huku wengine viumbe wakinawiri. Athari zaidi za ongezeko la joto Duniani, kama vile kupungua kwa theluji milimani, kupanda kwa eneo la bahari lenye maji, na mabadiliko ya hali ya hewa, yanaweza kuathiri si tu shughuli za kibinadamu bali hata mfumo wa kiikolojia. Kusoma kuhusu uhusiano kati ya hali ya anga ya Dunia na kuangamia kwa viumbe katika kipindi kilichopita cha miaka milioni 520, wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha York wanaandika, \"Vipimo vya joto Duniani vilivyotabiriwa kwa karne zinjazo vinaweza kusababisha ‘tukio jipya kubwa la maangamizi ya viumbe’, ambapo zaidi ya asilimia 50 ya spishi za wanyama na mimea itaangamizwa.\"",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nKuanzia mwaka wa 1961 hadi mwaka wa 2003, vipimo vya joto vya bahari Duniani kote vimeongezeka kwa kiwango cha 0.10 °C kutoka eneo la juu la bahari hadi urefu wa mita 700 ndani ya bahari. Kuna tofauti kuanzia mwaka mmoja hadi mwingine na hata vipindi virefu zaidi vya wakati, huku joto la Duniani kote la bahari likipanda kati ya mwaka wa 1991 hadi mwaka wa, lakini kupoa kukirekodiwa kati ya mwaka wa 2003 hadi mwaka wa 2007. Kipimo cha joto cha eneo la Bahari ya Antaktiki ya Kusini kilipanda kwa 0.17 °C (0.31 °F) kati ya miaka ya 1950 na 1980, karibu mara mbili zaidi ya Bahari za Dunia kijumla. Ikijumuisha madhara ya mifumo ya kiikolojia (k.m. kwa kuyeyusha barafu ya baharini, kuathiri algae ambayo humea katika sehemu ya chini), kuongezeka kwa joto kunapunguza uwezo wa bahari wa kuchukua ndani CO.",
"Madhara ya ongezeko la joto duniani\nKulingana na jarida la mwaka 2003 la Smith na Hitz, ni jambo la busara kudokeza kuwa uhusiano kati ya ongezeko la kipimo cha joto cha wastani cha joto Duniani na uzalishaji wa kiikolojia ni wa kiparaboli. Ukolezi mwingi zaidi wa gesi ya kaboni daioksaidi kutasaidia mimea kukuwa na kutosheleza mahitaji ya maji. Mwanzoni vipimo vya juu vya joto vinaweza kusaidia ukuaji wa mimea. Hatimaye, ongezeko la ukuaji litafikia kilelel halafu litaanza kushuka. Kulingana na ripoti ya IPCC, ongezeko la kimataifa la joto linalozidi 1.5-2.5°C (ikilinganishwa na kipindi cha 1980-99), litakuwa na matokeo mabaya kwa mfumo wa kiikolojia, bidhaa na huduma, k.m., ugavi wa maji na chakula. Utafiti uliofanywa na Mradi wa Kiswidi kuchunga Miti ulipendekeza ya kuwa miti inayokuwa polepole hufanywa kuwa kwa kipindi kifupi chini ya viwango vya juu zaidi vya gesi ya CO, huku miti inayokuwa kwa kasi kama vile liana, hufaidika baada ya kipindi kirefu. Kwa jumla, lakini hasa katika misitu ya mvua, hili linamaanisha kuwa liana huwa ndiyo spishi inayopatikana kwa wigi; na kwa sababu liana huoza haraka kuliko miti kaboni anayopatikana ndani yao inarudishwa haraka zaidi angani, Miti inayokuwa polepole huweka kwa ndani kaboni ya annga kwa miongo mingi."
] | 24
|
Je, blogu ni nini?
|
[
"Blogu\nBlogu ni teknolojia mpya inayowezesha watu binafsi kuchapa maoni na fikra zao katika mtandao wa tarakilishi maarufu kama wavuti au intaneti. Blogu inaweza kuchukuliwa kama ni shajara pepe."
] |
[
"Nonini\nNonini (amezaliwa 1 Oktoba 1982) jina lake haswa ni Hubert Nakitare, ni msanii wa nyimbo aina ya hip hop kutoka nchini kenya awali akisajiliwa na calif records,lakini baadaye alijiunga na homeboyz productions. Yeye alijitosa kwenye ulingo wa muziki wa mijini nchini Kenya kupitia wimbo wake \"Nonini ni Nani?\" kupanda kwa umaarufu wake kitaifa na kikanda haukuanza hata hivyo mpaka alipotowa wimbo wake \"Manzi wa Nairobi\" mwaka 2002, wimbo ambao ulisifu uzuri wa wanawake wa Kenya na kufuatiliwa na wimbo \"Weh Kamu\". Yeye aliendelia kwa kutoa albamu yake \"Hanyaring game\" mwishoni mwa mwaka wa 2004 ambayo ilihusisha wimbo maarufu \"Keroro\" neno la kisheng lenye maana ya pombe ya bia.Nonini anajulikana kwa kutoa wimbo wa kwanza wa Genge",
"Agostino wa Hippo\nWewe ni nini kwangu? Uniwie huruma, niweze kusema.\nMimi ni nini kwako, hata uniagize nikupende,\nhalafu nisipokutii unanikasirikia na kunitishia maafa makubwa?\nJe, kutokupenda si balaa kubwa tayari?\nLo, kwa huruma yako, Bwana Mungu wangu,\nuniambie wewe ni nini kwangu.\n“Uiambie nafsi yangu, Mimi ni wokovu wako”.\nSema hivyo, nami nitasikiliza.\nTazama, moyo wangu unakusikiliza, Bwana; uuweke tayari ukaniambie,\n“Mimi ni wokovu wako”.\nNitafuata sauti ya neno lako hilo hata nikufikie.\nUsinifiche uso wako: nife nisije kufa, bali niuone uso wako.",
"Jay Rosen\nJay anaandika katika blogu yake iitwayo Pressthink ambayo inazungumzia juu ya taaluma ya uandishi katika zama za Intaneti. Pia huwa anaandika katika blogu ya The Huffington Post. Pressthink ilishinda tuzo ya Freedom Blog Award inayotolewa na shirika lisilo la kiserikali la Reporters Withouth Borders mwaka 2005.",
"Wimbi la Njaa\n\"Wimbi la Njaa\" ni jina la wimbo wa Juma Nature akiwa na kundi lake la F.S.G kutoka Temeke, Dar es Salaam, Tanzania. Wimbo umetoka mwaka 2000. Wimbo huu ni wimbo wa pili kurekdi akiwa na F.S.G na umepata kuonekana kwenye tepu ya kwanza ya albamu ya Juma Nature \"Nini Chanzo\". Baadaye ukaja kufanyiwa remix akiwa na KR Mullah na kuwekwa katika albamu tu. Wakati huu muziki kutoka TMK ulikuwa unapamba moto. Juma Nature aliinua TMK vya kutosha kuanzia 2000 hadi 2006. Ngoma kibao alipata kushirikishwa na wasanii wengi kutoka TMK na wengine mahali pengine pa Dar.",
"WordPress\nWordpress ni programu ambayo inawasaidia wenye blogu kuweka makala katika blogu zao kwa urahisi. Imetengenezwa na na . Programu hii ni ya bure yaani mtumiaji hahitaji kulipa chochote ili kuitumia. Huwa pia ni open source yaani kila mtu anaweza kuendeleza programu hii na kuiboresha zaidi. Kando na kutumika na wanablogu, wordpress pia hutumika na wenye jukwaa (forum) za kujadili mambo kadha wa kadha, wanaoweka picha za sanaa katika wovuti (media galleries) pamoja na wanaofanya mauzo kwa mitandao (ecommerce stores).",
"Nje ya Bongo\nNje ya Bongo ni jina la albamu ya nne kutoka kwa msanii wa muziki wa hip hop wa Dar es Salaam, Tanzania maarufu kama II Proud. Albamu imetoka mwaka 1999, mwaka mmoja tangu atoe albamu ya tatu. Nyimbo kali kutoka katika albamu ni pamoja na Deiwaka, Nje ya Bongo, Nipo Kwenye Microphone na Siku Yangu. Albamu imefanywa kipindi ambacho 2 Proud ndiyo mara yake ya kwanza kufanya safari ya Ulaya na kurekodi nyimbo hizo akiwa hukohuko barani Ulaya. Albamu imetayarishwa na Mongo Star amemtaja katika wimbo wa Nje ya Bongo, vilevile II Proud nae katia mkono katika kutayarisha albamu hii. Kifupi hakuna albamu ambayo 2 Proud hajashiriki katika kutayarishaji kasoro Coming of Age-Ujio wa Umri tu. Zilizobakia zote katia mikono yake. DJ Jumanne alisaidia katika kutayarisha albamu hii. Halafu kipindi hiki si zamani sana tangu J4 afanye utafiti wake wa muziki wa hip hop wa Tanzania.",
"Nonini\nBaadaye,wimbo Nani mwenza, kwa ushirikiano na mwanamuziki kutoka Tanzania Juma Nature, uliweza kujulikana kikanda. Katika ubunifu mkubwa hivi karibuni,ameshirikiana pamoja na msanii Nameless kuunda wimbo wa kitaifa wa Ijumaa ujulikanao kama \"furahi day\" ambao umechezwa sana katika vituo vya utangazaji. nyimbo zote mbili ziko kwenye albamu yake ya pili Mwisho Ya Mawazo,iliyotolewa mwaka 2007. Albamu yake iliwahusisha wanamuziki wakiwemo Nyota Ndogo, Mercy Myra, Profesa Jay na Q-Chief Agosti 2007, Nonini alikuwa miongoni mwa Wakenya 100 wenye ushawishi mkubwa kama ilivyochanguliwa na gazeti la The Standard Nonini alishinda tuzo bora la kimuziki la Chaguo La Teeniez mwaka 2008 kwa video yake ya \"Mtoto Mzuri\" katika Mwaka wa 2009 alitajwa kama Balozi wa international Lifestyle na Chuo Kikuu cha Limkokwing nchini Malaysia",
"Eric Shigongo\nLengo la kitabu ni kwamba tubadilikeː je, wewe ungekuwa mwanadada huyo ungefanya nini?",
"Nini Chanzo (wimbo)\n\"Nini Chanzo\" ni jina la wimbo wa sita kati ya nyimbo 11 zinazopatikana kutoka kwenye tepu ya kwanza ya albamu ya \"Nini Chanzo\" na wa kwanza kwa upande B kutoka kwa msanii wa muziki wa hip hop kutoka nchini Tanzania, Juma Nature. Wimbo umetayarishwa na P. Funk ndani ya Bongo Records. Wimbo huu ndio pekee kutoka katika albamu ambao umejihusisha na masuala mbalimbali ya kisiasa ya Tanzania na nchi nyingine za Afrika. Nature anajaribu kuelezea hali halisi ya siasa ya Afrika na hila zake. Jinsi wanasiasa wanavyoweza kuingiza watu mkenge kwa manufaa, huku wakifahamu fika atakayeteseka ni mwananchi wa kawaida wakati huo yeye yupo uhamishoni anakula nchi. \nKwa siasa ya Tanzania, ambayo tangu imeanza mabadiliko yake ni machache sana. Hasa ukizingatia awali ilikuwa siasa ya vyama vingi, lakini miaka ya 1960 kumetokea mabadiliko mengi kwenye uwanja wa siasa hasa kwa kufuatia mkanganyiko na mvurugano wa kiongozi wa juu na wale wa chini ambao waliamini wamepigania uhuru na kuanzisha vyama vyao vya kupambana katika chaguzi mbalimbali. Ili kuondoa fujo za kisiasa kwa wakati ule wa miaka ya 1960, ilikuwa kuna ulazima wa kusitisha vyama vingi kwa muda hasa kwa kufuatia uchanga wa nchi na malumbano tena, kwa busara, babu akaona ngoja kwanza. Sasa mwenyekiti wa chama ndiye Rais wa nchi, kama ilivyo sasa japo tangu 1992 siasa imekuwa ya vyama vingi na kumetokea mabadiliko mengi kwenye uwanja huo lakini si urais, ambapo mwenyekiti ndiye rais. Mstari wa kwanza tu anaanza:\n\"Rais sio msaliti tumekuchagua kuwa mwenyekiti,\nKwenye suala la uongozi umetuonesha kwamba uko fiti\"\nHalafu anatoa angalizo:\n\"Lazima ukumbuke kuwa ukitenda dhambi zitakutafuna\"\n\"Kwa kuwa shukurani huna, ni vyema kufanya kazi kwa manufaa ya Afrika\"\nManeno haya ya Juma Nature yanaakisi siasa kubwa ya Afrika. Wapo viongozi waliofanya kazi kwa manufaa ya Afrika na dunia au Afrika ikafurahi. Japo kinafiki, lakini wamefurahi. Mmoja wapo ni kiongozi wetu Baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere. Baada ya Tanganyika kupata uhuru, hajakomea kwake. Kahakikisha majirani na baadhi ya Waafrika wenzake wanakuwa huru, ikiwa ni pamoja na Zambia, Afrika Kusini, Mozambique, Zimbabwe, Uganda na ushirika kiasi kwa chi jirani na Tanzania. Viongozi kama akina Ghadaffi ni miongoni mwa viongozi waliopendwa Afrika japo siasa za kuchafuana kutoka ughaibuni zilipelekea mambo kwenda kusi.",
"Hotuba ya mlimani\nJe, mtapata tuzo gani kwa kuwapenda tu wale wanaowapenda ninyi? Hakuna! Kwa maana hata watoza ushuru hufanya hivyo!"
] | 38
|
Je, Rhodesia ya Kaskazini ina jina gani kwa sasa?
|
[
"Cecil Rhodes\n1885 alifaulu kupata kibali cha serikali ya Uingereza kuanzisha koloni ya binafsi kaskazini ya Afrika kusini. Akaunda Kampuni ya Kiingereza ya Afrika Kusini (British South Africa Company) na kuvamia maeneo ya Zambia na Zimbabwe ya leo. Ardhi iliyotwaliwa iliuzwa kwa walowezi na koloni za kampuni ziliitwa Rhodesia ya Kaskazini na Rhodesia ya Kusini. Zilikaa chini ya kampuni ya Rhodes hadi 1923 zikachukuliwa baadaye na serikali ya Uingereza.",
"Rhodesia ya Kaskazini\nRhodesia ya Kaskazini (kwa Kiingereza: Northern Rhodesia) ilikuwa jina la koloni halafu eneo lindwa la Uingereza katika Afrika ya Kusini lilipopata uhuru wake kwa jina la Zambia tarehe 24 Oktoba 1964.",
"Shirikisho la Afrika ya Kati\nShirikisho la Afrika ya Kati (liliitwa pia Shirikisho la Rhodesia na Unyasa) lilikuwa dola la kujitawala chini katika mfumo wa ukoloni wa Uingereza uliounganisha nchi za leo za Zambia, Zimbabwe na Malawi zilizoitwa wakati ule Rhodesia ya Kaskazini, Rhodesia ya Kusini na Unyasa (Nyassaland).",
"Kampeni za Kivita katika Afrika ya Mashariki (Vita ya Kwanza ya Dunia)\nKatika Septemba 1918 alipata habari ya kwamba Waingereza walikuwa nyuma yake kwa jeshi kubwa. Hapa aliamua kurudi Tanganyika na kuelekea Rhodesia kwa sababu habari zilimfikia ya kwamba Waingereza hawakuwa tena na jeshi huko. Tarehe 28 Septemba alivuka tena mto Rovuma akaendelea katika sehemu za kusini kupitia Songea na Mbozi. Mwezi wa Novemba aliingia Rhodesia ya Kaskazini (Zambia). Tarehe 13 Novemba kikosi chake kiliteka mji wa Kasama ambako Waingereza wachache walikimbia walipomwona. Siku iliyofuata afisa Mwingereza alikaribia kambi yake na kumletea habari ya kwamba vita ilikwisha tayari na Ujerumani iliwahi kusimamisha mapigano yote tangu 11 Novemba 1918. Lettow alipatana na Waingereza kuongoza askari hadi mji wa Abercorn (leo Mbala, Zambia) aliposalimisha amri tarehe 23 Novemba 1918.",
"Rhodesia ya Kusini\nKoloni liliundwa na Cecil Rhodes aliyetwaa eneo hili pamoja na \"Rhodesia ya Kaskazini\" au Zambia na kuliweka chini ya Kampuni ya Kiingereza ya Afrika Kusini (British South Africa Company)."
] |
[
"Rhodesia ya Kaskazini\nPande zote mbili ziliunganishwa chini ya kampuni kama \"Northern Rhodesia\" mwaka 1911.\nMwaka 1923 serikali ya Uingereza iliamua kuchukua utawala mikononi mwake. Rhodesia ya Kusini ikawa koloni lenye kiwango cha kujitawala kwa ajili ya walowezi Wazungu wa huko. Rhodesia ya Kaskazini lilikuwa na walowezi wachache tu, ikawekwa chini ya idara ya makoloni ya Uingereza kama nchi lindwa kuanzia 1924 hadi uhuru mwaka 1964. Kampuni ya Kiingereza ya Afrika Kusini iliendelea kibiashara hasa kuchimba madini kwenye migodi ya kanda la shaba hadi uhuru uliolazimishwa kukabidhiwa mali yake kwa serikali ya nchi huru.",
"Harare\nMji ulianzishwa mwaka 1890 BK kama kambi la jeshi la binafsi la Cecil Rhodes. Tangu kuwa makao ya kudumu mji ulipewa jina la Salisbury kutokana na Lord Salisbury aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza miaka ile akamsaidia Cecil Rhodes kazika mipango yake ya kupanusha ukoloni katika Afrika ya Kusini. Salisbury ilipata cheo cha mji mwaka 1935 ikawa mji mkuu wa Maungano ya Rhodesia na Unyasa mwaka 1953 hadi 1963.\nBaada ya uhuru wa Zimbabwe jina la Salisbury ilibadilishwa mwaka 1982 kwa heshima ya chifu wa Washona Neharawa kuwa Harare.",
"Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania\nKipindi cha kwanza kilikuwa 1977-78 wakati jeshi la Rhodesia iliingia ndani ya Msumbiji. Rhodesia (leo:Zimbabwe) ilitawaliwa wakati ule na serikali ya walowezi Wazungu chini ya Ian Smith. Warhodesia walijaribu kuangamiza vikundi vya wapinzani kutoka kwao waliotafuta kupindua serikali ya walowezi wakijificha katika Msumbiji na kushambulia kutoka huku. Hapo vikosi vya Rhodesia viliingia mara kadhaa ndani ya Msumbiji halafu Rhodesia ilianzisha harakati ya Renamo kwa kukusanya wapinzani dhidi ya Frelimo na kuwapa silaha. Baada ya kuenea kwa vita ndani ya Rhodesia jeshi lake lilishambulia kambi kubwa ya wapinzani chini ya Robert Mugabe katika Mkoa wa Manica wa Msumbiji. Hapo Tanzania ilituma wanajeshi wake kwa shabaha ya kuimarisha utawala wa Frelimo wakarudi kwao mwaka ufuatao 1978.",
"Rhodesia ya Kaskazini\nMfalme wa Walozi katika magharibi alifanya mkataba wa ulinzi na Waingereza mwaka 1890 kwa imani ya kwamba ushirikiano na kampuni ya Rhodes ungehifadhi ufalme wake dhidi ya Wareno na Wangoni. Wabemba waligawanyika kati yao wakakosa wakati ule uwezo wa upinzani. Magharibi ilitawaliwa kama \"North Western Rhodesia\".",
"Saida Karoli\nKujulikana kwake kwa kasi nchini Uganda kulisababishwa na matumizi ya lugha ya Kihaya, lugha inayofanana zaidi na lugha ya Kiganda inayotumika na Waganda wengi, sauti nyororo na ya kuvutia na vionjo kibao vya kuvutia vya kijadi katika nyimbo zake.\nMnamo mwezi Juni mwaka 2003 Saida akatoa albamu nyingine nzuri iliyokwenda kwa jina la Mapenzi Kizunguzungu na kuweza kuteka soko la muziki tena kwa mara ya pili kutokana na vionjo kama vya awali vya kijadi.",
"Rhodesia ya Kusini\nRhodesia ya Kusini lilikuwa jina la koloni la Uingereza katika nchi ya Kusini mwa Afrika iliyopata uhuru kwa jina la \"Zimbabwe\" tangu mwaka 1980."
] | 23
|
Je, ziwa Nakuru lina ndege gani maarufu?
|
[
"Ziwa Nakuru\nZiwa Nakuru, ziwa ndogo yenye maji ya chumvi kusini mwa mji wa Nakuru inapatikana takriba kilomita 160 kutoka Nairobi. Hivyo basi inaweza kutumbelewa katika ziara ya siku moja kutoka mji mkuu.Au zaidi, kama sehemu ya mzunguko inayohusisha Masai Mara au Ziwa Baringo na Samburu mashariki. Ziwa hili ni maarufu sana duniani kama eneo kubwa ya kusanyiko ya ndege aina ya flamingo ambayo idadi yao ni zaidi ya milioni moja- ama hata milioni mbili!Wao hula mwani, ambayo hupatitakana kwa wingi katika ziwa hili.",
"Ziwa Nakuru\nMbuga ya kitaifa ya Wanyama ya Ziwa Nakuru (188 km ²), ilianzishwa mwaka 1961 kuzunguka Ziwa Nakuru, karibu na mji wa Nakuru . Inajulikana sana kwa maelfu, wakati mwingine mamilioni ya ndege aina ya flamingo yanayokusanyaka ufuoni mwa ziwa Nakuru. Ya usawa wa ziwa vifupi recog Idadi ya flamingo katika ziwa hutegemea maji na hali ya chakula na pahali bora kuwatazama ni juu ya kiinuko kinachoitwa Baboon Cliff. Eneo lingine lenye kivutio ni eneo la 188 km ambalo limezingirwa kwa ukuta wa seng'enge kuhifadhi wanyama walio na hatari ya kuangamia kama twiga , Kifaru mweusi na Kifaru mweupe",
"Ziwa Nakuru\nWingi wa mwani katika ziwa hili huvutia kwa kiasi kikubwa ndege aina ya flamingo ambayo hupatikana sana katika ufuo wa ziwa hili.",
"Ziwa Nakuru\nZiwa Nakuru ni mojawapo ya maziwa ya magadi katika Bonde la Ufa. Linapatikana kusini mwa mji wa Nakuru, katika eneo la kati nchini Kenya na linazungukwa na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Nakuru. Hifadhi hiyo ilianzishwa mwaka 1961. Ilianza ndogo, ikizingira ziwa hilo maarufu na maeneo ya milima yaliyo karibu. Na sasa imeongezwa kujumuisha sehemu kubwa ya maeneo ya mbuga.",
"Utalii nchini Kenya\nMbuga ya wanyama ya kitaifa ya Ziwa Nakuru, lililoanzishwa mwaka wa 1961 karibu na Ziwa Nakuru, liko karibu na mji wa Nakuru. Inajulikana sana kwa maelfu, na wakati mwingine mamilioni ya ndege wa aina ya flamingo wanaokusanyika ufuoni mwa ziwa Nakuru. Wajihi wa ukame wa ziwa hili ni vigumu kujulikana kwa sababu ya flamingo wengi. Idadi ya flamingo katika ziwa hutegemea maji na hali ya chakula. Pahali bora kuwatazama ndege hawa ni juu ya mwinuko unaoitwa \"Baboon Cliff\"."
] |
[
"Ziwa Nakuru\nFlamingo hula mwani ambayo hotokana na mchanganyiko wa kiniesi chao pamoja na maji ya chumvi yaliyo vuguvugu pamoja na chakula cha samaki aina ya plankton. Lakini flamingo sio ndege wa kipekee wa kuvutia kwenye ziwa hili, kunao ndege wala samaki wa aina ya pelican na cormorants.Licha ya maji haya kuwa ya chumvi na vuguvugu,samaki aina ya Tilapia grahami imeonekana kunawiri baada ya kuwekwa mwanzo wa miaka ya 1960. Ziwa hili lina ndege wengi sana. Kuna zaidi ya spishi 400 kwenye ziwa hili na mbuga iizungukayo. Maelfu ya ndege wa aina nyingine pia huonekana. Kunao pia punda milia.",
"Chocheeni Kuni\nUBETI WA PILI:\nMngekuwa mnajua anachokula nyuki, msingethubutu kusema asali ni tamu\nNiwashukuru, kwa kufikiri mjini ni hifadhi yenu\nHalikuwa wazo baya kwa wakati ule\nMaana mlionyesha ukomavu kutoka kwenye shingo kwenda chini na sio juu\nMbona hamkumfikiria aliyekuwa ndani kafungiwa kwa nje?\nUsingizi hapati anawaza jinsi ya kutoka\nNikisema uwezo wa watu kufikiri na mahitaji unatofautiana,\nmtaanza kusema nina dharau na matusi\nLakini kumbukeni ulimi unauma kuliko meno\nMnawezaje kumfikiria aliyekuwa ndani,\nkajifungia mwenyewe, funguo anazo mwenyewe,\nKalala fo fo fo, asijue hata idadi ya misumari iliyoshikilia mlango wake\nKulipamba jeneza, hakumfanyi aliyekufa kufufuka nyinyi\nKama kusema nimeshasema sana, mwishowe nitakuwa kama mwanasiasa\nHawajitokezi mpaka kuwe na maafa",
"Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Nakuru\nHifadhi ya Taifa ya Ziwa Nakuru ni mbuga ya wanyama nchini Kenya iliyoko kando ya Ziwa Nakuru, karibu na mji wa Nakuru. Umbali wa Nairobi ni km 140. Geti kuu liko kilomita 4 kutoka mji wa Nakuru. Eneo lake ni takriban km² 188. Inajulikana hasa kwa wingi wa ndege aina ya heroe na kundi la vifaru ambao wanaonekana hapa kwa uhakika mkubwa kulingana na mbuga nyingine za Kenya.",
"Mshale wa Mungu\nKitabu hiki kimeandikwa katika mazingira ya vijiji vya Waigbo wa Nigeria. Ezeulu ni kuhani mkuu wa mungu Ulu, anayeabudiwa na vijiji sita vya Umuaro. Kitabu hiki kinaanza na Ezeulu na Umuaro kuanza vita na kijiji jirani cha Okperi. Mgogoro huu unatatuliwa mara moja wakati TK Winterbottom, mwangalizi wa kikoloni wa Uingereza anapoingilia.\nBaada ya vita, mmisionari Mkristo, Yohana Goodcountry, anafika Umuaro. Goodcountry anawasimulia wanavijiji hadithi za Wanigeria katika Niger Delta ambao wameacha (na kuzipinga) \"mila zao mbaya,\" na kupendelea Ukristo. Kwa kuamsha ghadhabu za jamii yake ya kitamduni, Ezeulu anamtuma mwanawe kujifunza kwa Goodcountry.\nEzeulu anaitwa mbali na kijiji chake na Winterbottom, na anaalikwa kuwa sehemu ya utawala wa ukoloni, sera inayojulikana kama kiwakala. Ezeulu anakataa kuwa \"chifu wa mzungu\" na\nanatupwa gerezani. Katika kijiji cha Ezeulu, watu hawawezi kuvuna vikuu kabla hajaidhinisha, lakini, kwa hasira ya kuwa gerezani, anakataa. Vikuu vinaanza kuoza mashambani na kupelekea njaa. Riwaya huitwa \"Arrow of God\" kwa sababu Ezeulu hujilinganisha na mshale katika upinde wa mungu. Anadai kuwa matatizo ambayo ameyaleta kijijini ni mapenzi ya Ulu. \nWengi wa wanakijiji tayari wamepoteza imani yao katika Ezeulu. Mwana mwingine wa Ezeulu anaaga dunia katika sherehe za kitamaduni, na wanakijiji wanatafsiri hii kama ishara kwamba Ulu amemwacha kuhani wao. Badala ya kukabiliana na njaa tena, wanakijiji wanageuka na kuwa Ukristo.",
"Nakuru\nMwaka 2006, mbunge wa wakati huo, Mirugi Kariuki aliuawa katika Marsabit wakati ndege aliyosafiria ilipata ajali. Ajali hii pia iliwaua wanachama wengine tano wa bunge. Uchaguzi uliandaliwa punde baada ya mazishi uligombewa na mwanawe William Kariuki Mirugi wa chama NARC-Kenya ambaye alishinda. Katika umri wa miaka 27, William Kariuki Mirugi akawa mmoja wa wajumbe wadogo kiumri wa bunge kuwakilisha Nakuru Town Constituency."
] | 38
|
Taifa la Kenya lilipata uhuru mwaka gani?
|
[
"Uchumi wa Kenya\nMiaka kumi na tano ya Uhuru wa Kenya, kama ilivyokua miaka iliyopelekea uhuru, ilitawaliwa na sifa zilizomhusu Jomo Kenyatta miongoni mwa watu. Utawala wa Kenyatta uliofikia kikoma mnamo Agosti 1978, wakati kitabu hiki hakijakamilika, unaelezewa kwa ufasaha na. Kinaelezea mchango aliokuwanao Rais huyo katika muelekeo wa Kibepari (capitalist) na kijamaa (socialist) unaodhihirika katika mikakati ya kiuchumi nchini Kenya hivi sasa.\nUshawishi wa ari ya “kinyakuzi” enzi za Kenyatta ulikuwa na athari zake. Jomo Kenyatta, muasisi wa Taifa la Kenya atakumbukwa daima kwa mchango wake katika kupatikana kwa uhuru nchini mwake. Hata hivyo, inasemekana kuwa uhuru wa Kenya ulikuja na matatizo chungu mzima: Ukabila, Rushwa, na Choyo. Nafasi za kiutawala zilipatikana kwa wachache waliokuwa na madhumuni ya kukusanya Utajiri mkubwa kadiri iwezekanavyo. Hata hivyo, mtizamo huu wa jinsi hali ilivyokuwa, unakingana na jinsi hali halisi ilivyokuwa. Je? Hakukuwa na ukabila kabla ya uhuru? Kiukweli, Jomo Kenyata hakuwa muanzilishi, bali mdhibiti mkuu wa hali ya kikabila nchini humo. Ulikuwepo na bado upo japo kuwa unadhihirika katika ngazi fulani fulani. Miezi ya mwanzo ya utawala wa Rais Daniel Arap Moi, ilitawaliwa na bidii za dhati za kutaka kuondoa makosa yote yaliyojidhihirisha katika utawala uliotangulia na kwa bahati mbaya, ulikuwa ni wakati mbaya na mgumu kiuchumi nchini Kenya. Hata hivyo, mawazo ya kuwa matatizo yote yangeweza kuisha kufumba na kufumbua, yalikosa msingi pamoja na uzuri wa matokeo yaliyokusudiwa na kwamba ukabila na rushwa ambavyo hupatikana ulimwenguni kote, vingeweza kupotea. Ni rahisi sana kulaumu nyakati zilizopita kuwa ni sababu ya matatizo ya sasa na ni rahisi pia kufikiri kuwa mambo mazuri yanaweza kupatikana kwa haraka. Kukubali matatizo yaliyouandama uongozi wa Kenyatta, sio kukataa mazuri yalo ambatana nao. Hatua kubwa zilipigwa kimaendeleo ya jamii ya watu wa Kenya miaka kumi na tano baada ya uhuru, bila kuzingatia baadhi ya maandiko yanayoweza kuwa yameandikwa nchini Kenya na kitabu hiki, kinalenga kutoa ukweli na uhalisia wa mambo.",
"Mlima Kenya\nMwaka 1963, katika siku ya uhuru wa Kenya, Kisoi Munayo alikita bendera ya Kenya juu ya mlima. Mwaka 1997, mlima Kenya uliteuliwa kuwa eneo la urithi wa dunia na UNESCO.\nHifadhi ya Taifa ya Mlima Kenya, ilianzishwa mwaka 1949. Inahifadhi eneo linalozunguka mlima. Awali ilikuwa hifadhi ya misitu. Tangu Aprili 1978 eneo limeteuliwa kama Hifadhi ya Mazingira ya dunia UNESCO .",
"Majeshi ya Ulinzi ya Kenya\nKatika alfajiri ya uhuru wa Kenya, Bunge la Taifa lilipitisha muswada (Miswada ya Kenya, 1963) kufanya marekebisho ya hadhi ya majeshi Kenya.",
"Kenya\nWaafrika walichaguliwa moja kwa moja katika bunge la uwakilishi kwa mara ya kwanza mwaka wa 1957. Licha ya Waingereza kutamani kuwakabidhi mamlaka wapinzani wasio na siasa kali ya Kiafrika, ni chama cha Kenya African National Union (KANU) kilichoongozwa na Jomo Kenyatta kilichounda serikali punde tu kabla ya Kenya kupata uhuru tarehe 12 Desemba 1963. Tarehe 12 Desemba 1964, Kenya ilipotangazwa kuwa jamhuri, Kenyatta akawa rais wa kwanza."
] |
[
"Ruwaza ya Kenya 2030\nRuwaza ya Kenya 2030 (Kiingereza: \"Kenya Vision 2030\") ni mpango wa maendeleo ya kiuchumi wa serikali ya Kenya kuendeleza maeneo mbalimbali ya kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya nchi. Malengo ya mpango kuzalisha ukuaji wa uchumi wa mwaka wa 10%. Hivi sasa, Kenya ina ukuaji wa Pato la Taifa 4.9% (2007). Maono haya yamefululizwa katika miaka mitano mitano ya mipango, mwanzo wake ukiwa 2008-2012. Mpango wa kwanza unaazimia uwekezaji katika sekta sita muhimu na miradi ishirini kabambe . Sekta zilizolengwa ni pamoja na utalii, kilimo, viwanda, biashara, teknolojia ya habari, na huduma za kifedha.",
"Jeshi la Anga la Kenya\nLilivunjwa baada ya mapinduzi yaliyoshindikana kufanywa na maafisa wa jeshi hili tarehe 1 Agosti 1982. Shughuli zake zilianzishwa tena na kudhibitiwa vikali chini ya jeshi lililojulikana kama 82 Air Force. Jeshi la Anga lilipata uhuru wake tena mwaka 1994.",
"Huduma ya Vijana kwa Taifa\nMwaka 2013, serikali ya Rais Uhuru Kenyatta ilianza mageuzi ya huduma ili kutatua ukosefu wa hali ya juu wa ajira kwa vijana nchini Kenya. Huduma iliyorekebishwa ilizinduliwa mwezi Septemba 2014. Iliruhusu makurutu kutoka vikundi vya jamii ambao waliruhusiwa kuajiriwa na shirika hili bila kupata mafunzo ya kijeshi.",
"Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kenya\nMbuga ya Taifa ya Mlima Kenya , iliyoanzisha mwaka wa 1949, hulinda kanda inayozunguka Mlima Kenya. Awali ilikuwa ni hifadhi ya misitu kabla ya kutangazwa kama mbuga ya kitaifa. Hivi sasa ni mbuga ya taifa ndani ya hifadhi ya misitu ambayo imeizunguka.Mnamo Aprili mwaka wa 1978 eneo hilo lilifanywa hifadhi ya Biosphere ya UNESCO. Mbuga ya taifa na hifadhi ya misitu ziliunganishwa zikawa katika orodha ya Urithi wa Dunia wa UNESCO mwaka wa 1997.",
"Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania\nTarehe 20 Januari 1964, bado wakati wa usiku, kikosi cha kwanza cha TR kwenye kambi la Colito Barracks mjini Dar es Salaam kiliasi na kujipatia silaha kutoka ghala. Maafisa Waingereza walikamatwa na kufungwa lakini mkuu Douglas aliweza kujificha. Waasi walivamia kituo cha redio, uwanja wa ndege, ikulu na ofisi ya posta na simu. Maafisa Waingereza na Waafrika wasioshiriki na waasi walisafirishwa Kenya. Rais Nyerere alienda mafichoni katika kanisa moja la kikatoliki ng'ambo ya bandari akamwachia waziri Oskar Kambona kazi ya kuwasiliana na wanajeshi. Madai ya wanajeshi yalikuwa kuachishwa kwa maafisa Waingereza na kupandishwa kwa mishahara. Siku za kwanza ya mgomo wa jeshi ilifuatwa na vipindi vya fujo mjini vilivyobadilika na vipindi vya kimya, mashambulizi dhidi ya maduka ya Wahindi na kukamatwa kwa Wazungu wachache. Hata mbalozi wa Uingereza alikamatwa kwa kipindi kifupi.",
"Kenya\nBaada ya uhuru, Kenya iliendeleza ukuaji wa kiuchumi haraka kupitia kwa uwekezaji wa umma, kuhimiza uzalishaji wa kilimo, na kushawishi uwekezaji wa watu binafsi na wageni katika viwanda. Pato la taifa lilikua kwa asilimia 6.6 kuanzia 1963 hadi 1973. Uzalishaji wa kilimo ulikua kwa asilimia 4.7 kila mwaka kwa kipindi hicho ukiwa umechochewa na ugawaji upya wa mashamba, kuanzishwa kwa kilimo cha mimea iliyoimarishwa, na kuanzisha mashamba mapya.",
"Kenya\nMswada wa ubinafsishaji umeidhinishwa ingawa kuanzishwa kwa tume ya ubinafsishaji hakujakamilika, mabadiliko katika utendakazi wa umma yametekelezwa na mwaka wa 2007 Kenya ilishinda tuzo la Umoja wa Kimataifa la Utendakazi wa Umma. Hata hivyo, kazi nyingi zinahitajika kufanywa ili kuiwezesha nchi hii kuyafikia mataifa yaliyoendelea sana kiuchumi, hasa yale ya Mashariki ya Mbali. Changamoto kuu ni pamoja na kuchukua hatua thabiti dhidi ya ufisadi, kupitisha sheria zinazoshughulikia ugaidi na biashara haramu, kutatua upungufu wa ufadhili wa bajeti kisha kurekebisha na kuunda miundo msingi. Inaaminika haya yatasaidia kudumisha sera za kimsingi za kiuchumi, na kuhakikisha ukuaji wa kasi wa kiuchumi uliofikia asilimia 7.2 mwaka wa 2007."
] | 18
|
Kenya ina kaunti ngapi?
|
[
"Kaunti za Kenya\nKatiba hiyo inaeleza kuwepo kwa kaunti 47 nchini katika mafungu 191 na 192, pamoja na ‘County Governments Act of 2012”. Kaunti hizi zilichukua nafasi za Mikoa ya Kenya. Mipaka ya kaunti iliwekwa kulingana na mipaka ya wilaya za kenya zilizokuwa zimeanzishwa kisheria mwaka wa 1992."
] |
[
"Mkoa wa Kati (Kenya)\nMkoa wa Kati (Central Province) ni mkoa wa Kenya unaoenea kati ya Mlima Kenya, Nairobi na Nyahururu. Eneo lake si kubwa lakini kuna msongamano mkubwa wa watu kulingana na mikoa ya jirani kwa sababu ya hali ya hewa na rutba ya ardhi inayolisha watu wengi. Nairobi iko nje ya mkoa.",
"Kenya\nNairobi inaendelea kuwa kituo muhimu na cha kimsingi kwa mawasiliano na biashara cha Afrika Mashariki. Kinajivuna kuwa na miundo msingi ya uchukuzi na mawasiliano bora zaidi katika eneo hili, na wafanyi kazi wenye ujuzi. Makampuni mengi ya kigeni hudumisha matawi yao katika eneo hili ama ofisi za kuyawakilisha mjini Nairobi. Mnamo Machi 1996, Marais wa Kenya , Tanzania na Uganda waliifufua Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC). Shabaha za EAC ni pamoja na kasawazisha kodi na ada zinazotozwa bidhaa, utembeaji huru wa watu na kuimarisha miundo msingi katika eneo hili. Nchi hizi tatu za Afrika Mashariki zilitia saini mkataba wa Customs Union Agreement mwezi wa Machi 2004.",
"Kaunti za Kenya\nUtendaji wa kaunti una wajibu wa kutekeleza madaraka ya serikali ya kaunti. Gavana ndiye mtendaji mkuu na husaidiwa na naibu wa gavana. Kila kaunti ina kamati ya utendaji iliyoundwa na:Kazi ya utendaji ni:Kila kaunti ina bunge. Wajumbe huchaguliwa kutoka wadi za kaunti katika uchaguzi mkuu. Pia, kuna wajumbe wa kuteuliwa ambao huwakilisha vikundi vilivyotengwa, vijana na kwa ajili ya kusawazisha uwakilishi wa jinsia. Wajumbe hutumikia kwa muhula wa miaka mitano. Bunge huongozwa na spika ambaye hafai kuwa mjumbe.",
"Mto Naipuki\nMto Naipuki ni korongo linalopatikana katika kaunti ya Marsabit, kaskazini magharibi mwa Kenya (eneo la Bonde la Ufa la Afrika Mashariki).",
"Kenya\nKenya ina eneo kubwa wanapoishi wanyamapori likiwemo Masai Mara, ambapo nyumbu na wanyama wengi walanyasi hushiriki katika uhamaji kila mwaka. Uhamaji huo, hasa uhamaji wa nyumbu, hutokea Juni hadi Septemba na hushirikisha mamilioni ya wanyama. Tukio hili huwavutia sana wapigaji picha za sinema. Takribani nyumbu 250,000 huangamia kila mwaka katika uhamaji huu wa kutafuta lishe wakati wa kiangazi.",
"Kaunti ya Nyeri\nTopografia ya kaunti huwa na miinuko mikali na mabonde. Mlima Kenya hupatikana katika mpaka wa Meru na Nyeri. Mto Chania na Mto Sagana ni mito mikubwa ambayo hupitia katika kaunti hii.",
"Mkoa wa Kati (Kenya)\nMkoa wa Kati ni kitovu cha kilimo cha Kenya. Kuna kahawa nyingi pia mazao mengine. Maziwa na bidhaa kutokana na maziwa kama vile jibini hutengenezwa hasa mkoani. Soko zake ni pamoja na mji mkuu wa Nairobi ulio nje ya mkoa mwenyewe lakini imepakana nayo.",
"Kaunti ya Kirinyaga\nMlima kenya na msitu unaouzunguka uko kaskazini mwa kaunti. Theluji ambayo huyeyuka kutoka Mlima Kenya hutengeneza mito, k.v. Mto Thiba na Mto Kiganjo. Mito mingine iliyo katika kaunti hii ni Mto Sagana, Mto Nyamindi, Mto Rupingazi, Mto Thiba, Mto Rwamuthambi and Mto Ragati.",
"Mto Kipa (Kajiado)\nMto Kipa (Kajiado) unapatikana katika kaunti ya Kajiado nchini Kenya (eneo la Bonde la Ufa la Afrika Mashariki).",
"Jiografia ya Kenya\nEneo hili la milima ndilo la juu zaidi nchini Kenya (na la pili kwa urefu barani Afrika): Mlima Kenya, unaofikia urefu wa mita 5,199 (futi 17,0570) na ni eneo lenye mito ya barafu. Ng'ambo ya mpaka wa Tanzania Mlima Kilimanjaro () huweza kuonekana upande wa kusini."
] | 11
|
Je,mto mkubwa gani zaidi bara Afrika ni?
|
[
"Kinshasa\nMto Kongo ni mto mrefu wa pili katika Afrika baada ya Nile, na ni mkubwa zaidi katika suala la kutoa maji. Kama njia ya maji, hutumiwa kusafiri kwa kiasi katika bonde la Kongo, na unaweza kusafiri kati ya mito ya Kinshasa na Kisangani, na matawi yake mengi yanaweza kusafiriwa. Mto ni chanzo muhimu cha umememaji, na kusini mwa Kinshasa unaweza kuzalisha nguvu za kutosheleza matumizi kwa bara zima.",
"Zambezi (mto)\nZambezi ni kati ya mito mirefu ya Afrika ikiwa na nafasi ya nne baada ya Nile, Kongo na Niger. Ni mto mrefu wa Afrika wa kuingia Bahari Hindi. Beseni lake lina km² 1,570,000 au nusu ya mto Nile. Chanzo chake iko Zambia inapita Angola mpakani na Namibia, Botswana, Zambia na Zimbabwe kwenda Msumbiji inapofikia Bahari Hindi katika delta ya 880 km².",
"Nile\nMto wa Nile (pia: Naili; kwa Kiarabu ,النيل an-nīl) ni mto mkubwa upande wa mashariki ya bara la Afrika. Mara nyingi hutajwa kuwa pia ni mto mrefu kabisa duniani kushinda mto Amazonas. Kutoka Ziwa la Viktoria Nyanza hadi mdomo wake kwenye Bahari ya Mediteranea Nile inavuka nchi za Uganda, Sudan Kusini, Sudan na Misri kwa urefu wa km 6,650."
] |
[
"Benue (mto)\nMto Benue (Kifaransa: Bénoué) ni tawimto mkubwa wa mto Niger. Chanzo chake ni katika nyanda za juu za Kamerun hasa milima ya Adamawa. Katika sehemuy a kwanza ya mwendo wake unatelemka mita 600 kwa mwendo kali. Karibu na mji wa Garua unaungana na mto Mayo Kébi. Baada ya mwendo wa 350 km mto unatoka Kamerun na kuingia Nigeria karibu na bandari ya Jimeta. Hapa mto una upana wa kilomita moja unaoweza kupanua wakati wa mvua. Baada ya Yola mto unapokea tawimto wake muhimu zaidi mto Gongola.",
"Ngazija\nEneo la kisiwa ni 1012.9 km². Umbali wake na pwani la Afrika bara ni kilomita 400 hadi Msumbiji. Kijiolojia ni kisiwa changa kushinda visiwa vingine vya Komori. Mlima mkubwa ni volkeno hai ya mlima Karthala mwenye kina cha 2361 m juu ya UB. Eneo kubwa kwenye kaskazini halifai kwa kilimi kwa sababu ni mawemawe tu bila maji.",
"Delta ya barani\nKimsingi kuna aina mbili za delta ya barani:\nMto wa Okavango unakwisha baada ya kuvuka Afrika ya kusini magharibi kwa 1600 km katika jangwa la Kalahari (Botswana). Mikono ya delta na maziwa yamejenga mazingira yenye mimea na wanyama wengi katikati ya jangwa kubwa. Delta inavuta watalii wengi kila mwaka.",
"Afrika\nNchi kubwa ya Afrika ni Algeria na nchi ndogo ni funguvisiwa la Shelisheli katika Bahari Hindi. Nchi ndogo Afrika bara ni Gambia.",
"Afrika\nAfrika ni bara lenye joto kuliko mabara yote na asilimia 60 za uso wake ni maeneo yabisi au jangwa.",
"Rasi Agulhas\nRasi Agulhas (ing. \"Cape Agulhas\") ni mahali pa kusini zaidi pa bara la Afrika. Iko karibu na mji wa Agulhas katika Afrika Kusini. Iko karibu pia na Rasi ya Tumaini Jema iliyo maarufu zaidi.",
"Milima ya Ufa Mashariki\nMilima ya Ufa Mashariki ni safu mbili za milima ya eneo la Maziwa makubwa ya Afrika, katika nchi a Kenya, Uganda, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Burundi.\nInaitwa hivyo kutokana na uhusiano wake na Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki; safu ya magharibi ina: Milima ya Virunga, Milima ya Mitumba na Milima ya Rwenzori, wakati ile ya mashariki ina vilele vya juu zaidi katika bara zima la Afrika: Mlima Kilimanjaro (mita 5,895, sawa na futi 19,340) na Mlima Kenya (mita 5,199, futi 17,058). Kati ya milima mingine kuna Mlima Elgon kati ya Kenya na Uganda. Yote, isipokuwa Ruwenzori ina asili ya volkeno."
] | 41
|
Je,mwanamziki Beyonce alizaliwa lini?
|
[
"Beyoncé Knowles\nBeyoncé Giselle Knowles (alizaliwa 4 Septemba 1981), anayefahamika zaidi kwa jina moja Beyoncé ni mwimbaji wa R & B, mtunzi wa nyimbo, mtayarishaji wa rekodi, mwigizaji na mwanamitindo kutoka Marekani. Alizaliwa na kukulia Houston, Texas na alihudhuria shule mbalimbali zinazofunza sanaa. Pia alianza kushiriki katika mashindano ya kuimba na kucheza ngoma akiwa mtoto. Knowles alikuja kujulikana katika mwisho wa miaka ya 1990 kama mwimbaji kiongozi wa kikundi cha wasichana cha R & B, Destiny's Child. Kulingana na Sony, mauzo ya rekodi za Knowles, yakiunganishwa na yale ya kikundi cha Destiny's Child, yamezidi milioni 100."
] |
[
"Abeti Masikini\nElisabeth Jean Finant (9 Novemba 1954 - 28 Septemba 1994) alikuwa mwanamuziki maarufu wa dansi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Alitambulika sana kwa jina la kisanii kama Abeti Maskini na Afrika Mashariki alijulikana sana kwa kuimba Kiswahili, hasa ule wimbo wake wa \"Likayabu\" (Manjano na amdalasini). Abeti alikuwa chotara kama Jolie Detta, baba yake mzazi akiwa ni mchanganyiko wa Mkongomani na Mbelgiji. \nAbeti alikuwa fundi wa muziki akiwa katika umri mdogo sana ambao hakuna aliyetegemea hasa kwa jinsia yake. Mbali na hapo, alifanikiwa kuwawezesha wasanii waliokuja kuwa wakubwa baadaye, Mbilia Bel na Tshala Muana. Mbilia alikaa katika chungu cha Abeti na kupikwa vilivyo kuanzia kuimba hadi kunengua kuanzia mwaka 1976 hadi 1981. Tshala Muana yeye kuanzia mwaka 1978 hadi 1979. Yondo Sister alipikwa na Abeti katika mwaka 1986. Mwingine ni mwanamama Abby Surya (1984 - 1986).",
"Beyoncé Knowles\nBeyonce pia amekosolewa kwa sababu ya mitindo yake ya kucheza ngoma. Uimbaji wake katika kaburi la Rais wa zamani wa Marekani Ulysses S. Grant tarehe 4 Julai 2003 ulisemekana kuwa wa kisherati; wanafamilia wa Grant waliohudhuria walitoa maoni tofauti kuhusiana na jambo hilo.",
"Beyoncé Knowles\nKnowles pia amethiri wasanii mbalimbali ya kisasa. Mwimbaji wa Pop Rihanna imelinganishwa na yeye wakati mwandishi wa safu katika jarida la 'The Guardian', Amina Taylor, alimwita \"Bajan Beyoncé\", Mwimbaji kutoka Kanada wa aina sawa ya muziki, Keshia Chante, pia aliathiriwa na Knowles. Aidha, wimbo wa kwanza wa mshindi wa \"American Idol,\" Jordin Sparks, \"Tattoo\", na albamu yake ya kwanza zimesemekana kuwa \"Beyoncé-ish\"; baadhi ya wakosoaji walisema kuwa \"Tattoo\" inaweza kuwa \"imetolewa\" kutoka kwa wimbo wa Knowles wa \"Irreplaceable\". Stephen Thomas Erlewine kutoka Allmusic alisema kuwa nyimbo za mwimbaji wa Marekani Katharine McPHEE, kwenye albamu yake iliyokuwa na jina hilo zilikuwa na athari kubwa kutoka kwa muziki wa Knowles. Rowland aliathiriwa na sauti ya Knowles wakati wa kurekodi albamu yake ya pili, \"Ms Kelly.\"",
"Angelina Jolie\nTarehe 6 Julai 2006, Jolie ameanza kumlea mtoto yatima wa miezi sita kutoka Ethiopia, jina lake Zahara Marley Jolie-Pitt (Jina Halisi Zahara Marley Jolie), ambae wazazi wake walifariki na Ukimwi.\nZahara alizaliwa 8 Januari, 2005 kama Tena Adam.\nJolie akamchukua mtoto na kumpeleka kwenye ktuo cha kulea watoto yatima kilichopo Addis Ababa.",
"Beyoncé Knowles\nKatika makala iliyoitwa \"Born to Entertain\", Knowles, akishirikiana na waimbaji wa mitindo ya kisasa na ya kale, alipokea sifa kutokana na maonyesho yake kwenye jukwaa. Katika kutoa maoni yake kuhusu ziara ya 2009 I Am ...Tour, mwandishi Alice Jones wa jarida la \"The Independent\" anaandika, \"kumtazama Beyoncé akiimba na kucheza kunaweza kukakufanya kwa upande mmoja ushangae na kwa upande mwingine uhisi kutengwa. Yeye huchukua jukumu lake la kuburudisha kwa umakini hivi kwamba yuko karibu kuwa mzuri kupita kiasi. Gazeti la \"The New York Times\" linsema, \"kuna usanii wa kustaajabisha katika hamu yake ya kutaka kuburudisha\". Mwandishi Michelle Renee Harris wa jarida la \"South Florida Times\" anaandika, Knowles \"humiliki jukwaa kwa mikogo na nguvu zake zinazomtambulisha ... akionyesha uwezo wake wa kuimba bila kuruka noti hata moja, mara nyingi akiwa ameshughulikia kucheza ngoma kwa nguvu na umaarufu ... hakuna mmoja, si Britney, si Rihanna na si Ciara anayeweza kufanya hivyo-kifurushi kamili cha sauti, mitindo ya uchezaji ngoma na uwepo.\" Maoni haya yaliungwa mkono na mwandishi Lorraine Schwartz wa \"The Examiner,\" ambaye aliandika, \"Kwa muda wa chini ya mwaka, nimeona Madonna, Britney na Beyoncé ... [Beyoncé] ndiye alikuwa, kwa mbali, bora miongoni mwa wote watatu.\nWahakiki pia husifu maonyesho yake kwenye jukwaa. Katika kutoa maoni yake kuhusu mojawapo ya maonyesho ya mwimbaji huyu, mwandishi Jim Farber wa \"The Daily News\" anaandika \"Beyoncé alionyesha umaarufu mkuu. Wakati wimbo ulipokuwa ukiendelea, yeye aliimba kwa urahisi. Jinsi Beyoncé alivyotumia mwili wake ulizidisha hisia za furaha. Huku nywele zake zikiwa zimeshikwa kwa njia ya kuvutia, akitingisha kiuno chake na miguu mirefu kiasi cha kumfanya Tina Turner amwonee fahari, uwepo wa Beyoncé ulijenga uimbaji wake kikamilifu. Mwandishi Stephanie Classen wa \" Star Phoenix\" anatangaza \"Beyonce si mwimbaji wa kawaida ... kutoka mwanzo, mwimbaji huyu wa umri wa miaka 27 anayeimba kwa nguvu alipaa juu ya wanavitimbi wote, huku akitawala onyesho kama malkia asiye na asili ya kibinadamu. Hakuna kitu chochote isipokuwa nguvu za kiungu kinachoweza kuelezea sauti hiyo ...[ Beyonce] anaweza kuimba vyema kushinda mwimbaji yeyote mwingine wa pop hivi leo.\" Jarida la \"Newsday\" linaandika, \"Yeye anathibitisha kuwa si lazima uwezo bora wa kucheza ngoma na sauti nzuri zisiwe na mtu mmoja pekee ... Hakuna hofu ya mdomo-synching hapa.****kindly assist to translate",
"Beyoncé Knowles\nKnowles alizaliwa katika Houston, Texas, na ni binti wa Mathew Knowles, meneja mashuhuri wa rekodi, na Tina Beyincé, mtengenezaji wa mavazi na nywele. Babake Knowles 'ni Mmarekani mwenye asili ya Kiafrika na mama yake ni Mkrioli mwenye asili ya (Mwafrika Mmarekani, Mmarekani alisia, na Mfaransa). Knowles alibatizwa na kuchukua jina la mama yake la kati, kama ishara ya shukrani kwa mama yake na kuzuia jina hilo lisisahaulike, kwani ni wanaume wachache tu wa familia ya Beyincé wanaolitumia jina hilo. Babu na bibi wa mama yake, Lumis Albert Beyincé na Agnéz Deréon, walikuwa Wakrioli kutoka Louisiana.waliozungumza Kifaransa Yeye ni dada mkubwa wa Solange, mwimbaji - mtunzi wa nyimbo, na mwigizaji.",
"Beyoncé Knowles\nKnowles daima amekuwa akitambuliwa kama kiongozi wa Destiny's Child. Mwandishi Jon Pareles wa gazeti la \"The New York Times\" alisema kwamba Knowles ana sauti inayokitambulisha kikundi, huku akiandika kuwa sauti yake ni \"nyororo tena kali, pamoja na mtetemeko unaodumu na inayoweza kucharaza nyimbo za 'soul'\". Mwandishi James Anthony wa jarida la \"The Guardian\" alisema kuwa sauti yake ni tofauti na ya kasi, na iliyo na mbinu za kwikwi. Wakosoaji wengine walisifu anuwai yake na nguvu. Katika marekebisho ya albamu yake ya pili, \"B'Day\" , mwandishi Jody Rosen wa jarida la \"Entertainment Weekly\" aliandika \"Beyoncé ni mfumo wa dhoruba uliojigeuza mwimbaji. Katika albamu yake pekee ya pili, \"B'Day,\" nyimbo ziliwasili kwa mbubujiko mkubwa wa mdundo na hisia, huku sauti ya Beyoncé ikipasua kelele za matigo ya wimbo; wewe utahitajika kutafuta kwa mapana na marefu - pengine katika kumbi za Metropolitan Opera - kupata mwimbaji mwingine anayeimba kwa nguvu zaidi ya zake ...Hakuna mmoja - si R. Kelly, si Usher bila kuwataja wapinzani wake wa 'pop'- anayeweza kufikia uwezo wa Beyoncé wa kuivuta mistari yake dhidi ya mapigo ya hip-hop. Mwandishi Chris Richards wa jarida la \"Washington Post\" anaandika, \"Hata wakati ambapo yeye hafanyi vyema kimuziki, yeye hupaa juu ya waigaji wake. Yote yako katika sauti yake -chombo kilichozidi cha binadamu kilicho na uwezo wa kuimba wimbo wowote kwa mgong'ono wa kusisimua au mngurumo kamili-. Mchomo, kubeza, ashiki, mapambano-Beyoncé huimba kutoka pande hizi zote kwa uwezo mkuu. Jarida la \"Cove\" lilimworodhesha katika nafasi ya saba katika orodha yao ya \"Waimbaji 100 mashuhuri wa Pop\" (The 100 Outstanding Pop Vocalists), na kumpatia alama 48 kati ya 50 kutokana na vigezo kadhaa vikiwemo uwezo wake wa kuimba na ulinganifu wa sauti.\nMara nyingi Knowles amesemekana kuimba sana. Kama mtu anayejulikana kuendelea kujiboresha, yeye mara kwa mara hulinganishwa na wasanii kama Mariah Carey, ambao umaarufu wao wa kuimba umejulikana kupungua kutoka kwenye utamu wa nyimbo zao. Jarida la \"Eye Weekly\" linaandika, \"Hakuna swali kwamba Beyonce ni mmoja wa waimbaji bora wa pop, labda mmoja aliyebora miongoni mwa walio hai ... [Hata hivyo] ingawa uimbaji wake una busara, athari kwa jumla bado ni kama kupondwa kichwa kwa ngumi iliyo kwenye glavu ya mahameli.",
"Afande Sele\nSeleman Msindi au Afande Sele (amezaliwa tar. 24 Aprili 1976) ni msanii wa muziki wa hip hop na Bongo Flava kutoka Mkoani Morogoro, Tanzania. Amewahi kushinda tuzo ya (mkali wa ryhmes) mwaka [2003] kutokana na wimbo yake wa \"Darubini Kali\" aliyomshirikisha Dogo Ditto kwa sasa Lameck Ditto. Ni muasisi wa makundi ya 'Ghetto Boys' na 'Watu Pori', yaliozaliwa na kufia mjini Morogoro kwa kufuatana na alikuwa msanii wa kwanza kuujaza uwanja wa mpira wa miguu wa JAMUHURI mjini morogoro alipozindua albam yake ya kwanza ya 'MKUKI MOYONI'. Aliongoza kampeni ya maleria mwanzoni mwamiaka ya 2005 na 2007. Mwanzoni wa mwezi wa 11 mwaka 2012 alitangaza rasmi kufanya kazi kama kundi jipya la watu pori baada ya kufanya kazi na MC KOBA ambaye ni miongoni mwa waliokuwa wakiunda kundi la watu pori miaka ya nyuma. Afande Sele kwa sasa ana video ya wimbo wake Soma Ule ambayo imeongozwa na mtayarishaji Raph Tz (upcoming video director) aliyepewa heshima na msanii huyo kufanya video hiyo ambayo imekidhi maudhui ya wimbo.",
"Beyoncé Knowles\nKnowles ametaja wasanii mbalimbali ambao wameathiri mtindo wake wa kimuziki. Yeye alikua akiwa anasikiliza nyimbo za Anita Baker na Luther Vandross, na hatimaye akashirikiana na Luther Vandross, lakini mara nyingi yeye hutaja Michael Jackson kama aliyemfanya aimbe na shujaa wake. Yeye pia alianza kusikiliza muziki wa jazz uliombwa na Rachelle Ferrell, baada ya kuimba nyimbo za Ferrell wakati wa masomo yake ya sauti. Knowles amewataja wasanii kutoka Marekani waliomwathiri wakiwa ni pamoja na Tina Turner, Prince, Aretha Franklin, Whitney Houston, Janet Jackson, Selena, Mary J. Blige, Diana Ross, Donna Summer, Mariah Carey na mwimbaji kutoka Colombia Shakira."
] | 35
|
Jennifer Garner ana miaka mingapi?
|
[
"Jennifer Garner\nJennifer Anne Affleck, hasa hujulikana kwa jina lake la kuzaliwa kama Jennifer Garner (amezaliwa tar. 17 Aprili 1972), ni mwigizaji wa filamu kutoka nchini Marekani. Garner amejipatia umaarufu mkubwa kwa kucheza kwake kama kachero wa CIA, Sydney Bristow, katika kipindi cha mfululizo wa TV cha \"Alias\", ambacho kilikuwa kikirushwa hewani na televisheni ya ABC kwa misimu mitano ambayo ilianza kuanzia 2001 hadi 2006. Wakati anafanyakazi kwenye \"Alias\", amepata kucheza nyusika chache-chache kwenye mafilamu makubwa-makubwa kama vile \"Pearl Harbor\" (2001) na \"Catch Me if You Can\" (2002). Tangu hapo, Garner ameonekana kwenye nyusika kadha wa kadha akiwa kama mwigizaji mwandamizi vilevile mwigizaji mkuu kwenye mamiradi makubwa ikiwa ni pamoja na \"Daredevil\" (2003), \"13 Going on 30\" (2004) na \"Juno\" (2007). Ameolewa na mwigizaji na mwongozaji wa filamu Ben Affleck, ambaye kwa pamoja wameweza kujipatia watoto wawili wa kike."
] |
[
"Jennifer Garner\nGarner ni wa pili kuzaliwa katika familia ya watoto watatu wa kike waliozaliwa huko mjini Houston, Texas. Mama yake, Patricia Ann, alikuwa mwalimu wa lugha ya Kiingereza kutoka mjini Oklahoma, na baba yake, Bill John Garner, alifanyakazi kama mhandisi wa kemikali katika Union Carbide. Wakati alivyokuwa na umri wa miaka minne, kazi ya baba yake na Union Carbide iliwahamisha kuelekea mjini Princeton, West Virginia, na kisha baadaye mjini Charleston, West Virginia, ambapo Garner aliweka makazi hadi alipofikisha kipindi chake cha miaka ya chuo. Alimsifia dada yake mkubwa, Melissa Lynn Garner Wylie, ambaye anaishi mjini Boston, Massachusetts, kama chanzo cha mafanikio yake. Mdogo wake wa kike ni Susannah Kay Garner Carpenter.",
"Jennifer Garner\nMnamo tar. 19 Oktoba 2000, Garner ameolewa na mwigizaji Scott Foley, ambaye alikutana naye kwenye seti ya tamthili ya \"Felicity\" kunako 1998. Baada ya kutengana na Foley mnamo mwezi wa Machi 2003, Garner amefungua faili la talaka kunako mwezi wa Mei 2003, na kutaja tofauti zao ambazo haziwezi kupatanishwa, na wawili hao wakatalikiana rasmi kunako tar. 30 Machi 2004. Kufuatia kutengana kwake, Garner akaanza kutembea na mwigizaji-mshirika mwenzake kwenye \"Alias\" Michael Vartan kuanzia mwezi wa Agosti 2003 hadi Machi 2004.",
"Jennifer Garner\nMsimamo wa Garner kiukuaji ni pamoja na kwenda kanisani kila Jumapili, hapaki majipambo ya usoni wala vibikini, na kusubiri hadi angalau alivyofikisha miaka 16 aruhusiwe masikio yake kutobolewa, ambapo, baadaye alileta mzaha kidogo, kaifanya famili yake \"kuwa mbali kidogo na Uamish.\" Ameanza kuchukua masomo ya ballet akiwa na umri wa miaka mitatu hadi kipindi chake chote cha ujana, lakini hajajibidisha yeye mwenyewe ili kufikia kiwango cha ballerina wa kisasa. Garner alisoma katika shule ya George Washington High School ya mjini Charleston, West Virginia. Mnamo mwaka wa 1990, alijiunga na Chuo Kikuu cha Denison kilichopo mjini Ohio, ambapo alijikita zaidi katika masuala ya uigizaji na kufanya kazi kadha wa kadha kuhusiana na masuala ya utayarishaji na tamthilia. Baada ya kuhitimu chuoni Denison, ambapo alijiunga na umoja wa kina dada wa Pi Beta Phi, kunako mwaka wa 1994.",
"Jennifer Garner\nWakati fulani katikati mwa 2004, Garner ameanza kutembea na mwigizaji-mshirika wa katika \"Daredevil\" Ben Affleck na wawili hao walionesha uhusiano wao mbele ya kadamnasi wakiwa kama wapenzi waliohudhuria katika siku ya ufunguzi wa Boston Red Sox-World Series kunako Oktoba 2004. Tangu uhusiano wake na Affleck, kwanza akiwa kama demu wake na kisha baadaye kuwa mkewe.",
"Jennifer J. Kayombo\nJennifer J. Kayombo ni binti mwenye umri wa miaka 21, anasoma chuo kikuu akichukua masomo ya stashahada ya mipango ya miradi, usimamizi na maendeleo ya jamii, pia ni kiongozi wa vijana, mwanaharakati wa mambo ya wanawake; kwa sasa amethibitishwa na Umoja wa mataifa kama balozi kijana katika malengo endelevu.",
"John Garner\nJohn Nance Garner IV (22 Novemba 1868 – 7 Novemba 1967) alikuwa Kaimu Rais wa Marekani chini ya Rais Franklin Delano Roosevelt kuanzia mwaka wa 1933 hadi 1941.",
"F. Gary Gray\nAkiwa na umri wa miaka 24, Gray akaongoza filamu filamu yake ya kwanza, vichekesho vya mjini \"Friday\" akiwa na rapa-mwigizaji Ice Cube na Chris Tucker. Baadaye akaja kuongoza filamu ya \"Set It Off\", akiwa na Jada Pinkett na Queen Latifah. Kisha akaongoza \"The Negotiator\", ambayo imechezwa na mshindi wa tuzo za Acadamy Kevin Spacey na mmoja wa waliowahi kushindanishwa katika tuzo za Academy Award-Samuel L. Jackson, na hapo ndipo alipopata tuzo-2 ya mwongozaji na filamu bora 1998 katika Tamasha la Filamu la Acapulco.",
"Patrick Garcia\nAliwa na miaka 9, Garcia alianzia kwenye usaidizi wa kanisa la mtakatifu James Parish (Ayala), Alabang walipokuwa wakiishi. Amelitumikia kanisa kwa miaka kadhaa mpaka pale familia yake ilipohamia Frisco del Monte, Quezon City. Akiwa na miaka 13, dada yake alimshawishi kujaribu kuigiza. Alijaribu kwenye filamu ya \"Seprada\" (1994), na akapata nafasi ya kuigiza. Filamu ilikubalika na ilimtambulisha Garcia kwenye sanaa ya uigizaji nchini Ufilipino. Mwaka uliofuata, Garcia alishika nafasi tofauti-tofauti kwenye filamu na tamthiliya kama \"Gimik\", \"Araw-araw\", \"gabi-gabi\", na \"Asero\". 1996, alianza kuonja rasmi ladha ya mafanikio baada ya kujishindia tuzo ya \"Best Child Actor\" kutoka FAMAS Awards akiwa ni umri wa miaka 15, kutokana na kuigiza kama Ryan kwenye filamu Madrasta.",
"Jackie Joyner-Kersee\nJoyner-Kersee alihudhuria chuo kikuu cha Chuo Kikuu cha California huko Los Angeles, ambako alikuwa na nyota katika kufuatilia na shamba na katika mpira wa kikapu wa wanawake tangu 1980-1985. Alikuwa anaanza nafasi yake ya mbele kwa kila msimu wake wa kwanza wa tatu (1980-81, 81-82, na 82-83) pamoja na mwaka wake wa juu (wa tano), 1984-1985. Alikuwa na shati nyekundu wakati wa mwaka wa mwaka wa 1983-1984 kuzingatia heptathlon kwa Olimpiki ya Summer ya 1984."
] | 40
|
Nani alikuwa rais wa kwanza Urusi?
|
[
"Boris Yeltsin\nBoris Nikolayevich Yeltsin () (kwa herufi za Kirusi huita:Бори́с Никола́евич Е́льцин) (1 Februari 1931 - 23 Aprili 2007) alikuwa rais wa kwanza wa Urusi baada ya mwisho wa ukomunisti. Alitumikia taifa la Urusi kuanzia mwaka 1991 hadi 1999. Mikhail Gorbachev, alimtangulia Boris, wakati huo Urusi iliitwa Umoja wa Kisovyeti. Vladimir Putin amekuja baada ya Boris. Boris Yeltsin alikufa kwa ugonjwa wa moyo mnamo tarehe 23 Aprili mwaka 2007.",
"Historia ya Urusi\nMarais wa Urusi baada ya 1991 walikuwa Boris Yeltsin na Vladimir Putin.",
"Urusi\nMarais wa Urusi baada ya 1991 walikuwa Boris Yeltsin na Vladimir Putin."
] |
[
"Nani\nMechi ya kwanza ya Nani ya ligi kuu ya Uingereza ilikuwa katika mechi ya ufunguzi ya nyumbani, Manchester United ikiwa mwenyeji wa Reading tarehe 12 Agosti na Nani aliingia kama mbadala kwa Wayne Rooney, ambaye alipata jeraha la mguu. Manmo 26 Agosti 2007, Nani alifunga bao lake la kwanza la ushindani la Manchester United, bao la ushindi kutoka yadi 30 katika dakika ya 69 dhidi ya Tottenham Hotspur. Pia Nani aliandaa mabao muhimu kwa Louis Saha na Nemanja Vidic na kuruhusu Manchester United kuzicharaza Everton na Sunderland 1-0. Pia alifunga bao maarufu dhidi ya Middlesbrough, ambayo ilianzisha ushindi wa 4-1. Hii ilikuwa mechi ya kwanza ambayo ilidhaniwa kwamba Wayne Rooney na Carlos Tevez walionyesha ahadi ya kwanza ya kweli ya kufomu ushirikiano mzuri. Alirudi kwa klabu yake ya zamani, Sporting, katika mechi ya ligi ya Mabingwa barani Ulaya mwezi wa Septemba, ingawa ilikuwa mwenzake na mchezaji wa zamani wa Sporting Cristiano Ronaldo ambaye alifunga bao la ushindi katika ushindi wa 1-0.\nMnamo 16 Februari 2008, Nani alikuwa mchezaji bora katika mechi dhidi ya Arsenal katika raundi ya nne Kombe la FA, bao lake na pasi mbili alizoziandaa zilizosababisha mabao ziliisaidia United kushinda mechi hiyo 4-0 dhidi ya wapinzani wao jadi. Katika mechi hiyo, Nani alihusika katika ubishi pamoja na nahodha William Gallas wa Arsenal ambaye aliona kwamba Mreno alikuwa \"anamadharau\". Baada ya mechi, pia Arsène Wenger hakuwa amefurahishwa na kitendo cha Nani huku Gilberto Silva akisema kuwa Nani alikuwa na \"kuchwa kubwa (ujeuri)\".",
"Thomas Sankara\nMwaka wa 1966, rais wa kwanza wa Volta ya Juu, Maurice Yameogo, aliondolewa kupitia mapinduzi na kamanda wa jeshi, Sangoulee Lamizana, alichukua uongozi. Lamizana akaanzisha chuo cha wanajeshi mjini Ouagadougou, ambacho kilikuwa cha kwanza nchini. Sankara alisikia kwenye redio tangazo kwamba wanafunzi wa kwanza wa chuo hicho watachaguliwa kutoka waliohitimu shule ya upili. Alipohitimu, alikuwa mmoja wa waliochaguliwa. Wakati huo, alikuwa na umri wa miaka 17.",
"Nani\nNani alifunga katika dakika ya 10 katika FA Community Shield mwaka wa 2009, lakini United ilipoteza mechi hiyo kupitia mikwaju ya penalti kufuatia sare ya 2-2. Nani alijeruhiwa begani wakati wa mechi hiyo, ambayo awali ilitarajiwa kumweka hadi mwanzo wa msimu, lakini alipona na kuichezea Ureno dakika 17 dhidi ya Liechtenstein tarehe 12 Agosti, na kuanza mechi dhidi ya Birmingham City tarehe 16 Agosti. Ingawa aliandaa pasi lililomsababisha Wayne Rooney kufunga bao la ushindi katika dakika ya 34, Ryan Giggs aliingia kama mbadala wake baada ya nusu ya kwanza ya mechi. ] Kuondoka kwa Cristiano Ronaldo kwenda Real Madrid kulimaanisha kuwa kungekuwa na wachezaji wengi ambao wangetaka kuchukua majukumu ya “free-kick” na Nani alichapa na kufunga bao lake la kwanza la msimu wa 2009-10 kutoka kwa “free-kick” dhidi ya Wigan athletic, katika ushindi wa 5-0 ugenini.",
"Nani\nNani alikuwa mwanachama wa kawaida wa kikosi cha Kireno katika mechi za kufuzu kushiriki katika Euro 2008 UEFA, na alifunga bao moja kati ya mbili katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Ubelgiji tarehe 2 Juni 2007. Pia alimwandalia pasi safi mchezaji mwenzake Ricardo Quaresma aliyefunga bao katika mechi ya kirafiki dhidi ya Italia tarehe 6 Februari 2008. Fomu ya Nani kwa Manchester United wakati wa msimu wa 2007-08 hatimaye ilimwezesha kupata mwito kwa kikosi cha wachezaji 23 cha Luiz Felipe Scolari kwa ajili ya Euro 2008, pamoja na mchezaji mwenzake wa klabu Cristiano Ronaldo. Nadra alitumika katika kampeni hiyo, lakini aliweza kuanda pasi safi iliyomsababisha Helder Postiga kufunga bao baada ya kuingai katika dakika 15 za mwisho katika robo fainali dhidi ya Ujerumani tarehe 19 Juni 2008. Ureno hatimaye ilipoteza mechi hiyo 3-2.",
"Nana Akufo-Addo\nMwishoni mwa utawala wa kijeshi wa Jerry Rawlings alianza tena kuandaa chama kipya cha NPP kuanzia mwaka 1992. \nKuanzia mwaka 1996 hadi 2008 alichaguliwa mara tatu kuwa mbunge. Mwaka 1998 alijaribu kuwa mgombea wa urais kwa niaba ya chama cha NPP lakini hakufaulu. Aliendelea kumfanyia kampeni mgombea mshindi John Kufuor. Baina ya 2001 na 2007 alikuwa waziri katika serikali ya rais huyo, kwanza kama waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu, halafu kama Waziri wa Mambo ya Nje ya Ghana.",
"Nani\nNani mwanachama mwenye umri mdogo zaidi katika kikosi cha vijana wasiozidi umri wa miaka 21 katika mashindano ya vijana wasiozidi umri wa miaka 21 ya UEFA mwaka wa 2006. Alicheza mechi yake ya kwanza ya timu kuu ya Kireno tarehe 1 Septemba 2006 na alifunga bao katika kushindwa kwa Ureno kwa mabao 4-2 dhidi ya Denmark katika mechi ya kirafiki.",
"Nani\nNani alifunga katika mechi yake ya kwanza katika mechi ya kirafiki ya kabla ya msimu dhidi ya Shenzhen Shangqingyin, mechi ambayo United ilishinda kwa mabao 6 bila jibu. Pia alifunga katika mechi iliyofuata dhidi ya Guangzhou Pharmaceutical kwa kuinua mpira upande wa kulia wa lango kutoka upande wa kushoto wa eneo la penalti. Nani aliamua kuweka rekodi sawa baada ya ripoti zilipendekeza kuwa alikuwa amepigwa marufuku na Alex Ferguson kupiga \"Somersault\" yake ya kawaida akisherehekea mabao yake kwani ilihofiwa atajijeruhi. \"Hiyo siyo kweli\", alisema. \"Ferguson hajawahi kusema nami kuhusu suala hili na mimi nitaendelea kusherehekea mabao kwa njia hii. Mazungumzo yake na nami ni mazungumzo ya kawaida, kama mazungumzo ambayo anayo na wachezaji wote \".\nNani alicheza mechi yake ya kwanza ya ushindani ya Manchester United tarehe 5 Agosti 2007, akija kama mbadala katika Community Shield dhidi ya Chelsea. United ilipewa nyara baada ya kushinda mechi hii kupitia mikwaju ya penalti 3-0, kufuatia sare ya 1-1 katika muda wa kawaida. Hii ilifuatiwa na bao la tatu la Nani kwa klabu siku tatu baadaye, wakati yeye alifunga dhidi ya Glentoran.",
"Muna Lee (mwandishi)\nAkiwa kiongozi wa kupigania haki za wanawake, Muna Lee alifanya mchango muhimu katika harakati za kisasa za wanawake, hasa mapambano ya haki sawa. Alikuwa mwanzilishi wa Tume ya Wanawake ya Amerika Zote. Ilikuwa katika jiji la New York, alikokutana na mume wake wa baadaye, mshairi wa Puerto Rico na mwandishi wa habari aliyeitwa Luis Muñoz Marín, ambaye angekuwa gavana wa kwanza wa Pwetoriko wa kuchaguliwa kwa uchaguzi wa kidemokrasia. Walifunga ndoa mnamo tarehe 1 Julai 1919 na wakati wa muungano wao walikuwa na watoto wawili: binti mmoja Munoz Muna Lee (anayejulikana kama \"Munita\") na mwana mmoja Luis Munoz Lee. Muna alipewa talaka rasmi mnamo 15 Novemba 1946, miaka miwili kabla ya Luis Muñoz Marín kuandikwa katika vitabu vya historia alipochaguliwa kama gavana. Iwapo wangekuwa bado mume na mke, Lee angekuwa Mwanamke wa Kwanza wa kwanza wa kisiwa hicho cha Pwetoriko.",
"Nani\nNani alicheza mechi yake ya kwanza ya Sporting katika msimu wa 2005-06, alicheza mechi 29 na alifunga mabao manne. Katika msimu wake wa pili, alikuwa na idadi sawa kwani alicheza mechi 29 na alifunga mabao tano. Pia alicheza katika mechi sita za Ulaya na kufunga bao mara moja."
] | 56
|
Je,chama cha KANU kilianzishwa na nani?
|
[
"Kenya People's Union\nMnamo Machi 1966, mzozo ulitokea katika mkutano wa chama tawala KANU uliyofanya mlengo wa kushoto wa chama ukiacha chama hicho na kuanzisha KPU. KANU ilibadilisha sheria za uchaguzi kulazimisha wabunge waliyejiunga na KPU kutetea viti vyao katika uchaguzi mdogo. KPU iliweza kushinda hasa kwa Waluo Mkoani Nyanza pekee, huku waliyesimama kwingine wakishindwa na wanasiasa kutoka chama cha KANU ambacho wakati huo kilikuwa kikitawalwa na wanasiasa Wakikuyu .\nMwisho wa Chama hiki uliwadia wakati wa Ufunguzi wa Hospitali ya New Nyanza mnamo 25 Oktoba 1969. Wakati huo rais Jomo Kenyatta hakupendezwa na ufunguzi wa hospitali hiyo kwa vile ilijengwa na fedha za Soviet na ilionekana kama mradi wa Odinga. Hata hivyo Kenyatta aliongoza sherehe za ufunguzi wake ili kuimarisha umaarufu wake Mkoani Nyanza. Wajaluo walijulikana kuwa wenye hasira mno kwa kawaida, hasa kwa serikali tangu mauaji ya Tom Mboya miezi michache iliyotangulia, huku vidole vingi vikimwelekea Kenyatta. Maandamano yalianzishwa wakati wa sherehe hizo za ufunguzi wakati wafuazi wa KPU waliushanbulia msafara wa rais. Zaidi ya watu kumi waliuawa wakati walinzi wa Kenyatta walifunguaufyatuaji wa risasi dhidi ya waandamanaji hao. Odinga na maafisa wengine wa chama cha KPU walititiwa nguvuni siku mbili baada ya tukio hilo. KPU kilifutiliwa mbali mnamo 30 Oktoba 1969, huku Kenya ikibakia na Chama Kimoja.",
"Kenya African National Union\nChama kilianzishwa 1960 na wanasiasa waliyekuwa wanachama wa Kenya African Union ilichoanzishwa mwaka 1944 kwa jina la Kenya African Study Union. Jina likabadilishwa haraka kuwa \"Kenya African Union\" likabaki hivyo hadi 1952 KAU iliposimamishwa na serikali ya ukoloni. Mwenyekiti wa KAU ilipos ajiliwa alikuwa James Gichuru. Gichuru alipatiya kiti chake cha uongozi Jomo Kenyatta wakati Kenyatta aliporudi Kenya baada ya miaka 20 ngambo. Gichuru angerudia tendo hili wakati alipochaguliwa kuongoza KANU ilipofufuliwa kupigania uchaguzi ambayo ingekuwa 1963. Kenyatta angeendelea kuongoza hiki chama tangu mwaka 1960 hadi kifo chake 1978. Tangu Oktoba 1978 Daniel Arap Moi akawa kiongozi wa chama."
] |
[
"LDP (Kenya)\nLDP ilikuwa chama kidogo sana bila maana yoyote hadi 2002. Mwaka ule kulikuwa na farakano katika chama tawala cha KANU. Raila Odinga aliyewahi kujiunga katika KANU 2001 pamoja na wenzake wa chama cha NDP aliondoka tena baada ya rais Daniel arap Moi kumtangaza Uhuru Kenyatta kuwa mgombea wa KANU kwa ajili ya uchaguzi wa 2002. Wanasiasa wengine wa KANU kama vile Kalonzo Musyoka, George Saitoti na wengine waliosikitika hatua hii ya Moi walienda pamoja na Odinga wakajiita harakati ya pinde (Rainbow Movement). Kwa kusudi la kuingia katika uchaguzi walihitaji kuwa haraka na chama kilichoandikishwa. Wakaogopa kuandikisha Rainbow kwa sababu hawakuwa na uhakika kama serikali ya Moi ingewazuia au la. Hapa walijiunga wote na LDP kwa sababu ilikuwa imeandikishwa tayari.",
"Chocheeni Kuni\nNatoa katoni ishirini za sabuni ya unga, aliyekwambia wale wachafu nani?\nKasafisheni kwanza nyoyo zenu ndio mrudi kwa wananchi\nNdugu zangu, tawi kavu, kuanguka wala sio ajabu\nWakati wao wanatenganisha mavi ya panya kwenye unga\nNinyi chicheeni kuni zilizoloa, maji yapate moto ugali usongwe\nwakiwauliza, waambieni huu ni utani hehehe, Hapa kwetu tuna makabila 120, tunataniana\nWaliopo hatuwataki, wanaotaka hatuwaamini\nManeno siku zote yanauma na yanachefua ukijua maana yake\nKwa mfano neno la kitoto, mtoto kumwambia mtoto tunasema watoto wanacheza\nNeno la kitoto, mtoto kumwambia mkubwa tunasema mtoto anakuwa\nMtoto akisema babaa, ile ndege yangu,\nBaba hata kama huna baiskeli, utamwambia ikitua nitakuletea, ndio utaratibu\nLakini maneno ya kitoto, mtu mzima kumwambia mtu mzima mwenzie, kuna walakini\nMimi safari imenishinda, na sitaki tena kuulizwa kwanini",
"Orange Democratic Movement\nKatika mwaka wa 2007 muungano huu ulianza kutokuwa imara, ambapo makundi mengine yalijiondoa. Chama cha Uhuru Kenyatta KANU ndicho kwanza, kujiondoa mwezi wa Julai mwaka wa 2007 na kuunga kuchaguliwa tena kwa Rais Kibaki , ingawa baadhi ya wanasiasa binafsi kutoka KANU walibaki katika ODM. kutokana nakutoelewana kati ya Kalonzo Musyoka na Raila Odinga, chama cha ODM kiligawanyika katika makundi mawili katika katikati mwa mwezi wa August2007.. Kundi la Raila, ambayo pia ni pamoja naMusalia Mudavadi, William Ruto, Joseph Nyagah na Najib Balala walijiondoa kayika ODM Kenya kuchukua chama cha ODM ambacho kilisajiliwa na Mugambi Imanyara, wakati huo kundi la Kalonzo, likiongozwa na yeye mwenyewe na Dr Julia Ojiambo llibakia katika asili ODM - Kenya.",
"Michael Wamalwa Kijana\nKatika pilkapilka za uchaguzi wa mwaka 2002, walianzisha muungano wa kisiasa na Mwai Kibaki na Charity Ngilu ili kuja na upande wa kushinda. Baadaye Kalonzo Musyoka na Raila Odinga,walipogundua upande wao wa KANU ulikuwa umeelekea kupoteza, walibadili mrengo na kujiunga nao ili kufaidi na hali na watu kwa sasa kutoa changamoto kwa chama cha aliyekuwa rais wakati huo Daniel arap Moi, Kenya African National Union, Kenya African National Union (KANU). Muungano huu uliitwa National Rainbow Coalition (NARC), na ulipata ushinda mkubwa katika uchaguzi huo na Mwai Kibaki kama Rais. Wamalwa aliteuliwa makamu wa rais.",
"Orange Democratic Movement\nODM ilianzishwa na chama cha Uhuru Kenyatta, KANU na chama cha Raila Odinga, LDP, lakini chama cha KANU kiliweza kujiondoa, na waliobaki waligawanyika katika makundi haya mawili yanayoongozwa na Raila Odinga (ODM; ndio wengi zaidi) na Kalonzo Musyoka (ODM-Kenya). Sababu ya farakano ilikuwa suala la nani atakuwa mgombea wa urais upande wa ODM.",
"Kenya African National Union\nKatika uchahguzi wa 1963. KANU ilishinda vyama vya KADU na APP na kupata ruhusa ya kuunda serikali huru ya kwanza nchini Kenya. Mwaka iliyofuata wabunge wa hivi vyama walivuka sakafu na kujiunga na KANU. Kenya ikawa nchi ya utawala wa chama kimoja, yaani defacto. Mambo yaliendelea hivo hivo, isipokuwa muda mfupi kutoka 1966-69, mpaka 1982 mwaka katiba ya Kenya iliharirishwa kulingana na mfumo wa chama kimoja na KANU kuwa chama cha kisiasa cha pekee yaani dejure. Vyama vingine vilipigwa marufuku. Hali hii ilidumu hadi 1991 wakati serikali ya Moi ililazimishwa kukubali vyama vingi na badiliko la katiba tena.",
"Uchaguzi nchini Kenya\nBaada ya majadiliano na serikali ya Ukoloni ya Britain mnamo 1963, Serikali iliruhusu mfumo wa ‘’Kura moja kwa kila mmoja’’ mnamo 1963. Uchaguzi wa kwanza uliisha taratibu huku Jomo Kenyatta akichaguliwa kama Waziri Mkuu wa kwanza wa Kenya mnamo 1963. Mwaka uliofuata, chama chake cha KANU ilihariri katiba ya Kenya kumfanya Kenyatta Rais wa kwanza wa Kenya Chini ya uongozi wake, ushindani uliisha pole pole wakati vyama vya kisiasa vyote viliungana na, au kudhulumiwa na chama tawala cha KANU. ).. Hii ilipelekea kuundwa kwa mfumo wa chama kimoja nchini mnamo hata baada ya kifo cha Jomo Kenyatta mnamo 1978. \nKenya iligeuzwa rasmi kuwa nchi ya chama kimoja cha Kisiasa mnamo 1982 kufuatia mabadiliko ya katiba. \nBaada ya maandamano ya Saba Saba mnamo 1990, KANU ilijikunja na kuanza mikakati ya kurekebisha mfumo wa kisiasa. Mnamo 1992, kipengele ambacho kilikuwa kimeifanya Kenya kuwa na mfumo wa Chama Kimoja kilifutwa na Kenya ikarejea kuwa na Mfumo wa Vyama Vingi.. Uchaguzi wa kwanza chini ya mfumo huo ulifanyika mnamo 1992 huku wa pili ukifanyika mnamo 1997. Katiba ya Kenya haikuwa imerekebishwa kutosha ili kuendeha mfumo huu. Hata hivyo, mnamo 2002, shughuli za uchaguzi zilitajwa kuwa za haki na huru na Jamii ya Kimaataifa, huku KANU ilkipokeza mamlaka kwa chama cha National Rainbow Coalition (NARC)"
] | 24
|
Mhariri mkuu wa gazeti la NRC Handelsblad anaitwa nani?
|
[
"NRC Handelsblad\nKatika mwezi wa Februari 2006,\"NRC Handelsblad\" ilianzisha gazeti dogo la asubuhi la kuvutia wasomaji wasomi ambao hawawezi kusoma gazeti la kila siku. Mhariri Folkert Jensma alipoondoka, nafasi yake ilichukuliwa na Birgit Donker mnamo 12 Desemba 2006."
] |
[
"NRC Handelsblad\nNRC Handelsblad, mara nyingi hufupishwa kuwa NRC, ni gazeti la kuchapishwa kila siku.Gazeti hili huchapishwa jioni katika nchi ya Uholanzi na Kampuni ya NRC Media. Gazeti hili liliumbwa mnamo 1 Oktoba 1970 kutokana na muungano wa jarida la \"Nieuwe Rotterdamsche Courant\" na jarida la \"Algemeen Handelsblad\".Jarida la Algemeen Handelsblad llikuwa jarida kuhusu hesabu za kibiashara kwa jumla na jarida la Nieuwe Rotterdamsche Courant lilikuwa gazeti la Roterdam. Katika mwaka wa 2006, jarida la porojo, \"nrc•next\", lilianza kuchapishwa. Katika mwaka wa 2007, usambazaji wa \"NRC Handelsblad\" ulikuwa nakala 249,099 katika siku ya Jumatatu hadi Ijumaa na nakala 270,189 katika siku ya Jumamosi.",
"NRC Handelsblad\nGazeti la \"NRC Handelsblad\" lilianzishwa mnamo 1 Oktoba 1970, baada ya muungano wa gazeti la Amsterdam la \"Algemeen Handelsblad\" na gazeti la Rotterdam la \"Nieuwe Rotterdamsche Courant\". \"Nieuwe Rotterdamsche Courant\" lilianzishwa katika mwaka wa 1844 na Henricus Nijgh huko Rotterdam. Gazeti la \"Algemeen Handelsblad\" lilianzishwa katika jiji kuu la Amsterdam katika mwaka wa 1828 na J.W. van den Biessen. Wito wa jarida hili,\"NRC Handelsblad\" ni \"Lux et Libertas\"- hasa ukimaanisha Mwangaza (ikiashiria wakati wa kuzuzuliwa na kuerevushwa- yaani mwangaza unawafungua macho) na Uhuru.",
"NRC Handelsblad\nUsambazaji wa gazeti hili ulikuwa nakala 242,950 katika mwaka wa 2004(idadi chache kuliko usambazaji wa nakala 265,000 katika mwaka wa 2002). Jumla ya usambazaji wa magazeti ulikuwa 4,013,547 katika mwaka wa 2004.",
"NRC Handelsblad\nTangu mwaka wa 2001, mtindo wa Lexicon umetumika. Mtindo huu wa uchapishaji uliandaliwa na Bram de Does na hutumika katika gazeti hili. De Does alichora ,pia, na kuandaa mtindo maalum ya kutumika katika kuchapisha vichwa vya habari motomoto.",
"Business Line\nMhariri mkuu ni Bw. N. Ram na Mhariri Mshiriki ni Bw. K Venugopal. Mwandishi Mohan Padmanabhan huandika makala mengi katika gazeti hili.",
"Charles Njonjo\nNjonjo ni mwana wa Yosia Njonjo aliyekuwa mkuu wa kikoloni na kupokea shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Fort Hare katika Afrika ya Kusini. Baada ya uhuru wa Kenya mwaka 1963, Njonjo aliteuliwa Mwanasheria Mkuu. Njonjo aliandikisha Chama cha G.E.M.A, lakini hapo baadaye angekuwa mpinzani wa kikundi mnamo mwaka wa 1976 akawastaki baadhi ya wanachama wake pamoja na Kihika Kimani, Njenga Karume na uhaini - amri mara Rais nchini aligeuka na kutupilia hio kesi. Naye Mwanasheria Mkuu aliushikilia kazi yake hadi mwaka wa 1979. Mwaka huo huo alichaguliwa kuwa Mbunge wa jimbo la Kikuyu na mwaka wa 1980 aliteuliwa kuwa Waziri wa Katiba katika Serikali ya Daniel arap Moi. Mwaka wa 1983 alilazimishwa kujiuzulu, na akaacha maisha ya umma baada ya uchunguzi wa mahakama alihitimiza alikuwa ananyanyasa watu ofisini mwake huku ikiwa na madai kwamba alikuwa anajaribu kuchukua urais kutoka Moi.. Hapo mapema mwaka wa 1980 alikuwa mwenyekiti wa Idara ya Shirika la Afrika Mashariki ya Wanyama.",
"Star Tribune\nKatika mwezi wa Machi 2007, Par Ridder alipewa cheo cha Mchapishaji katika \"Star Tribune\" baada ya mchapishaji wa zamani, J. Keith Moyer, kuacha kazi yake baada ya \"Star Tribune\" kuuzwa. Ridder alijiuzulu tarehe 7 Desemba 2007. Ridder ni mwanachama wa familia ya Ridder iliyomiliki Knight-Ridder ,wachapishaji wa magazeti kadhaa kama vile (washindani wao) \"Saint Paul Pioneer Press\". Kuwasili kwa Ridder kulileta kesi ilipogunduliwa kuwa alikuwa ameiba kipande muhimu cha tarakilishi ya \"Pioneer Press\" cha kuhifadhi data kuhusu kampuni hiyo. Kipande hicho cha tarakilishi kilikuwa kimejaa habari kuhusu wafanyikazi wa kampuni hiyo na data ambazo \"Pioneer Press\" ilidai kuwa \"siri za kibiashara\". Ridder ,pia, aliajiri wafanyikazi wawili wa vyeo vya juu kutoka \"Pioneer Press\" alipoajiriwa na gazeti lile la Minneapolis. Hii ilileta ubishi kwa kuwa wafanyikazi hao wa vyeo vya juu huwa wamekatazwa ,katika mikataba yao na kampuni, kuajiriwa na kampuni zilizokuwa washindani wao kwa muda fulani. Mnamo 18 Septemba 2007, Ridder alitolewa kutoka kazi yake na hakimu wa kata la Ramsey. Hakimu huyo hamkukubalisha kufanya kazi huko tena hadi Septemba 2008.",
"Otago Daily Times\nSid Scales alikuwa mchoraji wa katuni wa gazeti la \"ODT\" kwa miaka 30 mpaka alipostaafu katika mwaka wa 1981. Tangu mwaka huo, mchoraji Garrick Tremain akawa mchoraji mkuu wa katuni wa gazeti hilo. Mhariri wa gazeti ni Murray Kirkness, aliyechukua hadhi hii kutoka mhariri wa muda mrefu, Robin Charteris mnamo Aprili 2007.",
"Ali Muhsin al-Barwani\nSheikh Ali alikua Mhariri Mkuu wa gazeti la \"Mwongozi\" kwa muda wa miaka kumi na tano. \"Mwongozi\" lilikua gazeti la siasa na jamii na la dini, na lilikua maarufu gazeti hilo kwa kazi yake kubwa ya kudai haki za wananchi na kutapakaza misingi ya Kiislamu huko Zanzibar na sehemu mbali mbali za Afrika ya Mashariki"
] | 2
|
Mtindo wa muziki wa hip hop ulianzishwa na nani?
|
[
"East Coast hip hop\nEast Coast hip hop ni jina la fomu ya muziki wa hip hop ambao unaasili na kukuzwa mjini New York City, Marekani, mwanzoni mwa miaka ya 1970 na 1980. Mtindo huu ulianza kujulikana hasa baada ya wasanii wengine kutoka sehemu mbalimbali za Marekani na kuongezea staili tofauti. \nEast Coast hip hop ulifahamika sana kama ndiyo fomu halisi ya muziki wa hip hop.",
"Hip hop\nHip hop ni aina ya muziki unaoelezea aina ya usanii na utamaduni uliyotokana na jamii ya Wamarekani Weusi na Walatino kunako miaka ya 1970 mjini New York City, hasa katika kitongoji cha Bronx."
] |
[
"Ondoa Giza Kitaa\nNari anaona watu wana mawazo ya kijinga kiasi kwamba hata lililo mbele yao wanashindwa kuliona. Anarejea maneno ya \"Macho Ngumu Kuona\". Uwoga katika maisha haukufanyi kufanikiwa bali kukudumaza. Sio kwamba ukiwa muoga ndio utaenda peponi. Namna ya ufundishaji ambao sio rafiki kwa wasomeshwaji. Watu hawaelewi kitu. Bado kuna wengine wanajifanya watumikia hip hop kumbe ndio wanafiki wakubwa katika suala zima la kuiponda. Wanashangazwa pamoja na majungu yao ndio kwanza muziki unapaa. Wanabaki na maswali tu. Vilevile anarejea jinsi Kilimo Kwanza kilivyoshindwa kumsaidia mtu wa hali ya chini. Nari anachukizwa na marafiki bandia wanajiofanya wanaeneza upendo ilhali wanaeneza skendo.",
"Nash MC\nTamaduni ni lebo ambayo NASH alifanya nayo kazi kwa mafanikio makubwa sana. Kupitia Tamaduni Muzik waliweza kubadilisha na kutimiza nguzo karibia zote za hip hop zinavyotaka. Maoni ya NASH kuhusu Tamaduni Muzik ni kwamba ndio wao waliobadilisha mtazamo na mwelekeo mzimaa wa muziki wa hip hop ya Tanzania. Kupitia wao, tuliweza kuona kutolewa kwa albamu kwa sana hata kwa wasanii wachanga, kutoa kandamseto, kurudisha maonesho ya hip hop kukusanya wasanii “Kilingeni” huko Msasani Club.",
"Nash MC\nMwaka wa 2005 aliamua kukaa chini na kuanza kuusoma muziki wa hip hop nje ndani ili aujue unatakaje na upoje. Alisoma vitabu mbalimbali vinavyoelezea na kuchambua muziki wa hip hop. Kilichomfanya atake kujua ni kwamba, alifahamu kiasi tu, labda baadhi ya albamu. Lakini miiko ya hip hop na misingi yake alikuwa haifahamu. Mwaka wa 2006 alikuwa ameanza kwiva sasa. \nAnakutana na kina mkubwa Zavara wa KU Crew, mtayarishaji Lindu kwa pamoja walimweka chini mdogo wao na kumpa madini ya hatari katika kufanikisha suala zima la kuzama ndani ya maisha ya hip hop. Lindu amegonga ngoma kibao ikiwa ni pamoja na Kimbia ya Babuu wa Kitaa, Wakati Ndio Huu, Natubu ya Chidi Benz na ngoma nyengine kibao.",
"Nash MC\nHii ni asili ya tangu enzi na enzi kwa muziki wa hip hop kuchukua sampuli ya nyimbo aidha za dance, pop, classic ballad na nyenginezo na kuzitumia katika muziki wa hip hop. Muungano huu wa Nash na Palla, unazua balaa kubwa katika tasnia. Wimbo ulipotoka ulileta sura mpya kwa wasikilizaji wa hip hop ya Tanzania. Nash anapata mahojiano rasmi ya kwanza na DJ Fetty wa Clouds FM. Mwaliko huo uliokuwa gumzo kituoni hapo kwa Nash kuongelea kwa kina dhima na nia ya hip hop katika jamii ya watu wa Tanzania kwa mapana yake.",
"Nje ya Bongo\nNje ya Bongo ni jina la albamu ya nne kutoka kwa msanii wa muziki wa hip hop wa Dar es Salaam, Tanzania maarufu kama II Proud. Albamu imetoka mwaka 1999, mwaka mmoja tangu atoe albamu ya tatu. Nyimbo kali kutoka katika albamu ni pamoja na Deiwaka, Nje ya Bongo, Nipo Kwenye Microphone na Siku Yangu. Albamu imefanywa kipindi ambacho 2 Proud ndiyo mara yake ya kwanza kufanya safari ya Ulaya na kurekodi nyimbo hizo akiwa hukohuko barani Ulaya. Albamu imetayarishwa na Mongo Star amemtaja katika wimbo wa Nje ya Bongo, vilevile II Proud nae katia mkono katika kutayarisha albamu hii. Kifupi hakuna albamu ambayo 2 Proud hajashiriki katika kutayarishaji kasoro Coming of Age-Ujio wa Umri tu. Zilizobakia zote katia mikono yake. DJ Jumanne alisaidia katika kutayarisha albamu hii. Halafu kipindi hiki si zamani sana tangu J4 afanye utafiti wake wa muziki wa hip hop wa Tanzania.",
"Nash MC\nAlipitia mengi yanayohitajika ili kuwa mchanaji hasa. Alipata msaada kutoka kwa wasanii wakongwe wa hip hop ya Tanzania kama akina Lindu Lindulu, Zavara Mponjika, Saigon na wengine wengi tu. Kwenye mwaka wa 2009 alifanya mahojiano ya nguvu na Saigon wakati huo mtangazaji katika kipindi cha \"HIP-HOP Base\" cha EATV. Mahojiano haya Nash aliongea mengi ya msingi kuhusu uwanja wa hip-hop na alivyorudi katika kuchana alikuwa tofauti na zamani kabisa. Baadaye akaja kutoa \"Nani Mkali Kwenye Game\" chini ya mtayarishaji Kita ndani Ramo Records huko Magomeni, Dar es Salaam. Hiyo ilikuwa mwaka 2010. Mwaka 2011 anatoa kandamseto ya kwanza \"Hazina Sura ya Kwanza\" halafu akaendelea kutoa albamu kila mwaka uliofuata hadi 2014. Mwaka wa 2012 \"Mzimu wa Shaaban Robert\", mwaka wa 2013 \"Chizi\", mwaka wa 2014 Mchochezi. Albamu zote zimetazamia maisha halisi ya raia wa Tanzania na Afrika kwa ujumla jinsi wanavyopitia magumu yao ya kila siku.",
"Nonini\nNonini (amezaliwa 1 Oktoba 1982) jina lake haswa ni Hubert Nakitare, ni msanii wa nyimbo aina ya hip hop kutoka nchini kenya awali akisajiliwa na calif records,lakini baadaye alijiunga na homeboyz productions. Yeye alijitosa kwenye ulingo wa muziki wa mijini nchini Kenya kupitia wimbo wake \"Nonini ni Nani?\" kupanda kwa umaarufu wake kitaifa na kikanda haukuanza hata hivyo mpaka alipotowa wimbo wake \"Manzi wa Nairobi\" mwaka 2002, wimbo ambao ulisifu uzuri wa wanawake wa Kenya na kufuatiliwa na wimbo \"Weh Kamu\". Yeye aliendelia kwa kutoa albamu yake \"Hanyaring game\" mwishoni mwa mwaka wa 2004 ambayo ilihusisha wimbo maarufu \"Keroro\" neno la kisheng lenye maana ya pombe ya bia.Nonini anajulikana kwa kutoa wimbo wa kwanza wa Genge",
"Bongo Flava\nBongo Flava ni jina badala la muziki wa Hip hop ya Tanzania. Mtindo huu ulianzishwa kwenye miaka ya 1990, hasa ukiwa kama mwigo au utokanaji wa hip hop kutoka Marekani, ikiwa na ongezeko la athira ya muziki wa reggae, R&B, afrobeat, dancehall, na mitindo ya asili ya Kitanzania kama vile taarab na dansi, muunganiko ambao umeunda mtindo wa pekee wa muziki. Mashairi kawaida huwa kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza.",
"Nash MC\nTamaduni Muzik laiti kama wangelikuwa wamesajiliwa au kutoa mikataba kwa wasanii, leo hii ingekuwa moja ya taasisi kubwa sana katika muziki wa Tanzania. Uzuri uliopo mahali ambapo shughuli za Tamaduni Muzik zilizokuwa zinafanyika ni karibu kabisa na ubalozi wa Marekani. Matukio yote walikuwa wanayaona, ila hila, urasimu na ubinafsi ulipo miongoni mwetu umepelekea kutopata msaada wowote kwa Tamaduni Muzik. Kifupi Tamaduni Muzik imehakikisha sanaa ya muziki wa hip hop inapata nafasi kubwa katika jamii ya Watanzania. Wameutetea mno muziki huu."
] | 42
|
Aina za tarakilishi ni ngapi?
|
[
"Tarakilishi\nKimsingi tarakilishi ni kifaa chochote kinachomsaidia binadamu kufanya hesabu. Zipo tarakilishi za aina mbili: za kianalojia (za umakanika) na za kidijiti (za elektroniki). Za kwanza \nhazitumii umeme, na ndizo ambazo zilianza kabla ya tarakilishi za kidijiti (zinazotumia umeme).\nKuna aina kuu tatu za kompyuta, nazo ni kama ifuatavyo:"
] |
[
"Amina\n\"Amina\" ni jina la kutaja wimbo uliotoka 2017 wa msanii wa muziki wa afropop kutoka nchini Kenya - Sanaipei Tande. Wimbo umetayarishwa na House of Dillie kwa maudhui ya kusikitisha ili kusindikiza midundo ya ndani. Ni moja kati ya nyimbo za huzuni sana kwa mwaka 2017. Sana ameonesha uwezo wa hali ya juu katika uimbaji tangu akiwa na bendi ya Sema hapo 2004/2005. Lakini kadiri anavyozidi kwenda mbele ndivyo uwezo unazidi kutamalaki. Wimbo umeonekana kuzungumzia maisha yake na usia kwa wasichana wasikate tamaa katika utafutaji wa maisha. Maisha yana mambo mengi, furaha, huzuni, matumaini, kusameheana, urafiki na kadhalika. Alitendwa kimahaba, hisia zake kaamua kuziweka katika wimbo. Dhumu la wimbo huu hasa ni kumuimbia binamu yake aliyefariki katika ajali ya gari akiwa anaelekea Mombasa kuposwa. Kupitia majonzi yake. aliweza kutunga wimbo wa kuenzi uhusiano wao.",
"Akwilina Akwilini\nAkwilina Akwilini Bafta (1 Aprili 1996 - 16 Februari 2018) alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha usafirishaji Dar es Salaam (NIT) ambaye alifariki baada ya kupigwa risasi ya kichwa kimakosa na afisa wa polisi aliyekuwa anajaribu kutuliza ghasia za waandamanaji wa kisiasa wa CHADEMA mnamo tarehe 16 Februari Ijumaa, 2018 huko Kinondoni. Tukio hili la kusikitisha limeamsha hisia kali sana katika mitandao ya kijamii nchini Tanzania. Wengi wamelaani kitendo cha askari kutumia risasi za moto kutuliza ghasia za kisiasa. Tena kwa watu ambao hawana silaha yoyote na wanafanya maandamano ya amani bila fujo. Baada ya tukio, kumekuwa na maswali mengi inawezekana vipi risasi iliyopigwa juu, impige mtu upande wa kushoto ubavuni itokee kulia. Baada ya tukio, polisi sita wahojiwa kuhusiana na tukio hilo la kusikitisha. Siku mbili tangu tukio kutokea, Rais wa Tanzania John Joseph Pombe Magufuli amelaani vikali tukio hilo lisilo la kibinadamu dhidi ya mwanafunzi huyo, na kuwataka wale wote waliohusika wafikishwe katika vyombo vya sheria. Baada ya hili kutokea, ukaanza msako wa kumtafuta mchawi aliyesababisha tukio hili, na hatimaye wakaungukia katika upande wa kisiasa. Hasa akina Mbowe na kikosi chake cha CDM kilichoshutumiwa kwa kufanya maandamano haramu yasiyo na kibali. Hata hivyo, viongozi wa juu wa CDM waliripoti polisi, na hatimaye kuachiwa kwa dhamana huku kukiwa na taarifa ya kwamba uchunguzi haujakamilika na wataitwa tena mara tu uchunguzi dhidi yao utakapokuwa tayari.",
"Nonini\nNonini (amezaliwa 1 Oktoba 1982) jina lake haswa ni Hubert Nakitare, ni msanii wa nyimbo aina ya hip hop kutoka nchini kenya awali akisajiliwa na calif records,lakini baadaye alijiunga na homeboyz productions. Yeye alijitosa kwenye ulingo wa muziki wa mijini nchini Kenya kupitia wimbo wake \"Nonini ni Nani?\" kupanda kwa umaarufu wake kitaifa na kikanda haukuanza hata hivyo mpaka alipotowa wimbo wake \"Manzi wa Nairobi\" mwaka 2002, wimbo ambao ulisifu uzuri wa wanawake wa Kenya na kufuatiliwa na wimbo \"Weh Kamu\". Yeye aliendelia kwa kutoa albamu yake \"Hanyaring game\" mwishoni mwa mwaka wa 2004 ambayo ilihusisha wimbo maarufu \"Keroro\" neno la kisheng lenye maana ya pombe ya bia.Nonini anajulikana kwa kutoa wimbo wa kwanza wa Genge",
"Abeti Masikini\nElisabeth Jean Finant (9 Novemba 1954 - 28 Septemba 1994) alikuwa mwanamuziki maarufu wa dansi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Alitambulika sana kwa jina la kisanii kama Abeti Maskini na Afrika Mashariki alijulikana sana kwa kuimba Kiswahili, hasa ule wimbo wake wa \"Likayabu\" (Manjano na amdalasini). Abeti alikuwa chotara kama Jolie Detta, baba yake mzazi akiwa ni mchanganyiko wa Mkongomani na Mbelgiji. \nAbeti alikuwa fundi wa muziki akiwa katika umri mdogo sana ambao hakuna aliyetegemea hasa kwa jinsia yake. Mbali na hapo, alifanikiwa kuwawezesha wasanii waliokuja kuwa wakubwa baadaye, Mbilia Bel na Tshala Muana. Mbilia alikaa katika chungu cha Abeti na kupikwa vilivyo kuanzia kuimba hadi kunengua kuanzia mwaka 1976 hadi 1981. Tshala Muana yeye kuanzia mwaka 1978 hadi 1979. Yondo Sister alipikwa na Abeti katika mwaka 1986. Mwingine ni mwanamama Abby Surya (1984 - 1986).",
"Nagharamia\n\"Nagharamia\" ni jina la wimbo uliotoka 19 Disemba 2015 wa msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Tanzania - Ali Kiba akiwa na mfalme wa masauti Christian Bella. Wimbo umetayarishwa na Abby Daddy ukiwa wimbo wa tatu kutolewa tangu kusimama kutoa kazi za kujitegemea miaka mitatu iliyopita. Vilevile huhesabiwa kama wimbo wa kwanza kumshirikisha mtu tangu kurudi kwake katika muziki mazima. Bella kafanya balaa zito humu kupita kiasi. Ujibizanaji baina ya waimbaji ni wa kipekee tangu Unanitega ya Noorah na Mwana FA na ya hivi karibuni iliyofanywa na Roma na Stamina Hivi Ama Vile. Video ya wimbo huu iliongozwa na Enos Olik kutoka Kenya na ndiye aliyekuja kuongoza video ya kucheza dansi la wimbo wa Sauti Sol wakiwa na Kiba Unconditionally Bae uliotoka Machi 10, 2016.",
"Anna Ndege\nMatokeo yake mazuri kuwahi kuyapata yalikuwa ni kushika nafasi ya kumi na tisa katika mashindano ya mbio fupi za mwaka 2001 (IAAF World Cross Country Championships). Ameiwakilisha Tanzania katika mashindano ya jumuiya ya madola mara mbili akiwa anashiriki mbio fupi za wanawake (IAAF World Cross Country Championships – Women's short race 2001 na 2002). Vile vile alishiriki katika mashindano ya jadi ya mwaka 2002 yaani kwa Kiingereza yanaitwa 2002 Commonwealth Games, Alishiriki kukimbia mbio zote za mita mia nane (800) na mita elfu moja mia tano (1500). Alikuwa mshindi mdogo wa medali hizo zilizoshindaniwa (Africa Military Games).",
"Adrian Siaga\nAdrian Adrian Siaga au Adiri (amezaliwa tar. 19 Januari 1975) ni mwigizaji wa filamu na tamthilia kutoka nchini Tanzania. Huenda akawa anafahamika zaidi kama Mhina kutoka katika filamu ya \"Zinduna\" iliyoshirikisha baadhi ya nyota maarufu kama vile Ashura Mushi, Emmanuel Mgaya, Mohammed Muki na Hussein Mkiethi. Vilevile Semwali kutoka katika filamu ya \"Kimela\" iliyoshirikisha nyota wengine kadhaa, Anna Peter, Mwasiti Madhohari, Juma Chete, Lilian Nyanza, Zubeiri Ramadhani na Faraji Mohammed. Adiri kutoka katika filamu \"Seuta II\" na Seuta II itimisho, Moses kutoka katika filamu ya \"Julia\" huku akiwa pamoja na Juma Chete, Mukasa Lawrence, Silvia Tairo, Leah Mussa, Shukuru Kilala, Bakari Abdallah, Abdul Mawazo, Winfrida Wilson, Emma Hassan, Paulina Edward na mwisho kabisa Hussein Mkiethi.",
"Niki Sanders\nTim Kring, mtunzi wa kipindi, alieleza ya kwamba awali alimuumba Niki akiwa na nguvu ya kuwa sehemu mbili kwa wakati mmoja, ambayo imetokana na maisha yake akiwa mama mlezi pekee. Niki pia awali alitungwa awe kama msichana wa onyesho. Hata hivyo, Ali Larter hakuwa na umbo la kuweza kucheza uhusika wa msichana wa onyesho, hivyo basi uhusika ukabadilishwa na akawa kahaba wa mtandaoni. Kwa mujibu wa watunzi Joe Pokaski na Aron Coleite, Niki alitolewa kwenye mfululizo na badala yake kawekwa Tracy Strauss hivyo Larter anaweza kucheza nyusika tofauti-tofauti, pindi walipogundua ya kwamba hawawezi kuendelea zaidi na uhusika wa Niki. Badiliko hilo lilipelekea kuweza kujua hadithi ya chimbuko lao, ambapo muhusika anagundua kwamba ana ngungu.",
"Ayi Kwei Armah\n\"Why Are We So Blest?\" (Mbona Tukabarikiwa Kiasi Hiki?) (1972) ina muktadha wake katika chuo ikuu cha Marekani, na mwanafunzi mwenye bidii, Modin Dofu, amewacha masomo yake katika Chuo Kikuu cha Harvad. Huku akiwa amekengeushwa akili yake imegawanywa kati ya uhuru na mitazamo ya Kimagharibi. Anakutana na mwanamke mweusi wa Kiportugal anayeitwa Solo, ambaye tayari amrukwa na kichwa, na mwanamke mweupe wa Kimarekani, Aimée Reitsch. Solo, mwandishi aliyekataliwa, anaandika kumbukumbu, ambayo ndiyo msingi wa riwaya yake. Tabia ya Aimée ya kutotangamana na watu na kujitolea kwake katika mapinduzi mwishowe kunasababisha maangamizi, ambapo Modin anwawa jangwani na Wanamapinduzi wa O.A.S.",
"Historia ya tarakilishi\nENIAC ilikuwa na ukubwa wa mita za mraba 167, uzito wa tani 27, na ilitumia umeme wa kilowati 150. Ilikuwa na maelfu ya Taa Ombwe, dayodi fuwele, rilei, kikinzanishi, na kapasita katika muundo wake.",
"Tarakilishi\nSehemu zinazoshikika (Hardware), ni aina zote za vifaa vya kompyuta, navyo vimegawanyika katika sehemu kuu tatu.Kibodi inatumika kwa ajili ya kuingizia herufi, namba, alama na michoro, nayo imegawanyika katika sehemu kuu nne, nazo ni kama ifuatavyo: Funguo za kuandikia (Typewriter keys), funguo za kuhama (Movement keys), funguo za namba pamoja na michoro mingine (Numeric keys) na funguo za kazi Function keys)."
] | 38
|
Je,mnyama mkubwa baharini ni yupi?
|
[
"Nyangumi\nOda nyingine ndogo ya Cetacea ni Mysticeti, ambayo hujumuisha nyangumi wa bluu, ambaye ndiyo mnyama mkubwa kuliko wote aliyeripotiwa kuishi, nyangumi mwenye nundu, na wanyama wengine wanaokula kutoka kwenye maji ya baharini kutumia michirizi mirefu iliyopo badala ya meno, ambayo ndiyo walikopatia jina lao."
] |
[
"Daraja takatifu\nKutoa daraja kwa wanaume tu si kuwakosea haki wanawake, kwa kuwa hizo ni huduma zinazofaidisha wote. “Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye” (Lk 22:27). Mwenye daraja anahudumia Kanisa kwa kumwakilisha Yesu; hivyo anatakiwa kuwa mwanamume kama yeye mbele ya Bibiarusi wake. Kukubali mgawanyo wa majukumu maishani ni kusifu hekima ya Mungu aliyetuumba watu wa jinsia mbili tofauti ili kustawisha familia, jamii na Kanisa. “Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana... Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake” (1Kor 11:11; 12:27).",
"Muumba\nMungu akiwa wema mkuu na mwenye uwezo wote, hakuumba ubaya wowote. Tena kila anapovumilia ule uliosababishwa na viumbe vyenye hiari (malaika na binadamu) anaufanya uzae mema makubwa zaidi kwa njia tusizoweza kuzifahamu vizuri hapa duniani. “Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi maisha ya watu… Nanyi kweli mlinikusudia mabaya, bali Mungu aliyakusudia kuwa mema, ili itokee kuokoa taifa kubwa, kama ilivyo leo” (Mwa 45:4-5; 50:20).",
"Samia Yusuf Omar\nMwezi wa Aprili alifaulu kupata nafasi kwenye mashua iliyopangwa kuwapeleka wakimbizi 70 Italia kwa siri. Mashua iliishia petroli ikaelea ovyo baharini kati ya Lybia na Sisilia. Manowari ya Kiitalia ilikaribia na wakati mabaharia walirusha kamba kwa mashua ndogo kulitokea msongamano mkubwa pale na watu kadhaa walisukumwa na kuanguka kwenye maji. Samia alikuwa mmoja wao akazama na akafa.",
"Historia ya Wapare\njiwe likaitwa mkumba vana, pia na Mfinga ya Kikweni makutano ya kwenda Ugweno na Usangi linaitwa Lubegho ambapo ni aghalabu mtoto kupona kwani akiamka toka usingizini akijigeuza tu hudondoka toka kule ju hadi chini nakufa. Maajabu ni kwa mtoto mmoja aliye okotwa na Mzee Mgaya kule Ikamba na kumlea hadi akakuwa na kuwa Mtumishi wa Mungu jasiri na maarufu Marehemu Mchungaji Nathanaeli Mgaya. Hadi leo hii mawe hayo yapo.",
"Wabondei\nSiku ile ile mwali wa kike anachukuliwa anawekwa ndani akiwa na kungwi wake ambae kungwi huyu ndie anaekuwa akimfundisha mambo kadhaa awapo kwa mume wake, humo ndani kunakuwa na mtungi wa asali pamoja na ndizi kibungaa zilizoiva (Ndizi kibungaa ni zile ndizi ndogo ndogo ambazo wengine huziita bungala) Mwali anapowekwa ndani anakuwa na miko ambapo mwiko mkubwa hatakiwi kula chakula chochote wala kunywa kinywaji cha aina yoyote ile hadi zitimie siku tano, na hizo ndizi na asali amewekewa ili aweze kupimwa imani yake ijulikane kuwa kweli mke yule ni mvumilivu na ana huruma kwa mume wake? Kwa kua endapo mwali Yule atakula chochote kati ya vile alivyowekewa pale ndani basi mwanaume anaetaka kumuoa huko aliko analegea na kuanguka, Familia ya mume wakijua kuwa mwanamke amekula kabda ya siku tano wanakwenda kuwasema familia ya mke kuwa mwana wenu hana imani na mtoto wetu maana amekula na kupelekea mtoto wetu ameanguka, hapa mwanaume anakua na hiyali ya kumuoa Yule binti ama kumuacha. , Kwa upande wa mwanaume siku tano hizo nae pia anakuwa katika sheria ya kutokula, vilevile ilikua akila tu basi mke wake anaanguka.\nSiku ya tano inapofika ngoma za kibondei zinakesha, Asubuhi ndugu wa kwa mume wanakuja huku wakiimba Nkondo wakiwa na Fimbo na mapanga wanacheza mduara huku ngoma zikipigwa, Baada ya hapo mume anaingizwa ndani ili kuandaliwa huku nje inapigwa ngoma ya maumbu ambapo wanawake wawili mmoja anajifanya mwanaume na mavazi ya kiume mwengine anajifanya mwanamke, huyu mwanamke anakuwa amebeba kikapu kisha anaigiza kuwa anatoroka anaingia kwenye nyumba Fulani kisha huyu anaecheza kama mwanaume anajifanya akimtafuta mke wake, Kila nyumba anauliza “Jamani hamjamuona mke wangu hapa” wanamjibu “Hatuja muona” Baada ya kutafuta na kuuliza sana ndipo wanapomuambia tumemuona kaingia nyumba ilee..(Kaingia nyumba ida) Anamfuata anamuona anamshika mkono na kutoka nae huku wakipigiwa vigelegele (Igizo hilo kwenye Ngoma hii ya maumbu linawafundisha wanaume kuwa mke akitoroka usimsuse, mtafute umrudishe).",
"Oyani\nOyani ni wadogo (mwili wa sm 30 na mkia wa zaidi ya sm 30) lakini wembamba wenye miguu mifupi. Rangi yao ni aina ya njano na wana mabaka meusi (madoa, milia) na mkia una zingo nyeusi. Huishi mitini na hukiakia usiku. Hula vitu vyingu kama wanyama na ndege wadogo, wadudu, matunda, koko na machipukizi ya mimea.",
"Jeromu\nAlimuandikia padri Neposyani: “Soma mara nyingi Maandiko ya Kimungu; tena, afadhali mikono yako isitue kamwe Kitabu kitakatifu. Jifunze humo unachotakiwa kufundisha… Usibandukane hata kidogo na mafundisho ya mapokeo uliyofundishwa, hivi kwamba uweze kuhubiri kadiri ya imani sahihi na kupinga wanaoikanusha… Matendo yako yasiachane kamwe na maneno yako, isije ikatokea kwamba unapohubiri kanisani mtu aweze kujisemea, ‘Mbona basi mwenyewe hafanyi hivyo?’ Angewezaje kujadili mfungo mwalimu aliyeshiba? Hata mwizi anaweza kulaumu uroho; lakini katika padri wa Kristo, akili na maneno vinatakiwa kulingana”.",
"Chumo\nMajibu yanakuja alikuwa ana homa kali iliyopelekea mtoto kufariki. Kule baharini, Juma anafanikiwa kupata samaki mkubwa, lakini Yustus anamfanyia kwa kumtupia baruti katika mtumbwi wake ili apoteze maisha. Yustus anarudi nchi kavu na samaki mkubwa mmoja na wadogo wengi, anakutana na Mzee Ali na kuanza kuuliza habari za Amina. Ali anauliza Juma yu wapi, majibu ya Yustus yanamkatisha tamaa Mzee Ali na kumweleza hakuna sherehe mpaka Juma arudi. Punde Juma anatokea na samaki mkubwa kabisa, ikawa furaha kwa Mzee Ali. Kwa furaha, Mzee Ali anamwambia Juma lazima ukamuone Amina katika kliniki ya karibu. Huko kliniki, Amina anampa Juma taarifa juu ya kilichotokea katika homa yake. Anampa salam za masikitiko ya kwamba wamepoteza mtoto jambo lililotokana na kutohudhuria mapema kliniki pindi tu, unaposhika ujauzito. Waliombana misamaha na kusameheana. Filamu inaishia wawili hao wakiona ufukwenu mwa bahari ya Hindi na kuishi maisha ya furaha.",
"Mnandi-pwani\nMinandi-pwani ni ndege wa bahari wa jenasi \"Fregata\", jenasi pekee ya familia Fregatidae. Wana domo refu lenye ncha kwa kulabu, mabawa marefu na mkia wenye panda. Rangi yao ni nyeusi; jike ana tumbo jeupe na dume ana mfuko wa koo mwekundu ambao anaweza kumvimbisha ili kumvutia jike. Ndege hawa hawaogelei na watembea kwa shida, kwa hivyo wako hewani takriban saa zote. Wanaweza kukaa hewani hata zaidi ya wiki moja. Kama shakwe-waporaji, huonekana mara nyingi wakipora mateka kwa ndege wengine, lakini chakula chao hasa ni samaki, ambao huwakamata wakiruka, na kwa kiasi kidogo zaidi makinda ya ndege. Jike hutaga yai moja au mayai mawili juu ya mti au ardhini au juu ya mwamba wa pwani.",
"Ngai\nKama ilivyo katika makabila mengineo ya Afrika Ngai hutolewa kafara, ni muumba, anauwezo dhidi ya viumbe na hata vitu visivyo kuwa na uhai na kadhalika. makazi yake kulingana na hadithi ya asili ya Agikuyu ni mlima Kenya (Kirinyaga). Kulingana na hadithi hii, Ngai alimuumba Gikuyu na mkewe Muumbi. Akawapa eneo la Muranga kama makazi yao. Akawabariki na mabinti tisa, kisha akaumba vijana tisa wa kiume iliwawaoe walipobaleghe. Kizazi baada ya kizazi jamii ya wakikuyu ilichipuka kutoka kwa nyumba hizi tisa. Majina ya Nyumba hizi hufanana na yale ya mabinti wa Gikuyu."
] | 6
|
Mji mkubwa nchini Afrika Kusini unaitwaje?
|
[
"Afrika Kusini\nMji mkubwa ni Johannesburg. Majukumu ya mji mkuu yamegawiwa kati ya miji mitatu: Cape Town ni makao ya Bunge, Pretoria ni makao ya Serikali na Bloemfontein ni makao ya Mahakama Kuu.",
"Mji mkuu\nAfrika Kusini ina miji mikuu mitatu kikatiba: Pretoria ndipo makao makuu ya serikali, Cape Town ndipo makao makuu ya bunge, Bloemfontein ndipo makao makuu ya Mahakama Kuu.\nBolivia ina mji mkuu rasmi katika jiji la Sucre, lakini ofisi nyingi za serikali ya kitaifa zimehamia mji mkubwa wa nchi La Paz.",
"Cape Town\nCape Town ulikuwa mji mkubwa wa Afrika Kusini hadi kupatikana kwa dhahabu katika eneo la Johannesburg kuanzia 1887."
] |
[
"Afrika Kusini\nMji mkuu wa jimbo watajwa katika mabano.Hii ifuatayo ni miji/manispaa/majiji kumi yenye wakazi wengi zaidi nchini.\nAfrika Kusini ina mchanganyiko mkubwa wa watu. Waafrika asili ni asilimia 80.2, Machotara ni 8.8%, Wazungu ni 8.4%, Waasia ni 2.5%.",
"Kamembe\nMji wa Kamembe una uwanja wa ndege wa pili kwa ukubwa nchini Rwanda. Kupeana kwake mpaka na Bukavu, DRC na kukaa kwake karibu na Burundi kuliwavutiya wahamiaji wengi kutoka nchi zote hizi mbili ambao walifanya Kamembe kuwa makazi yao ya kudumu. Wengine wahamiaji waliokuwa Kamembe walikuwa waarabu ambao waliokuja na kukaa Kamembe aidha kama vile wakimbizi wa vita vilivyo wahi kuwa huko visiwa vya unguja ao wafanya biashara waliojihusisha na biashara ya bidhaa kama vile kahawa na ngozi wa n'gombe. Biasha ya bidhaa hizi ilinawiri sana katika myaka ya 1930 hadi mwishoni ya myaka ya 1970. Mchanganyiko huu wa raiya kutoka nchi jirani, uhamiaji wa waarabu na kunawiri kwa biashara ya bidhaa hizo zilizotajwa hapo kabla, kulifanya Kamembe kuwa na hali ya kipekee ukilinganisha na miji mingine ya nchini Rwanda.",
"Limpopo (mto)\nChanzo kipo katika milima ya Witwatersrand, kati ya Pretoria na Johannesburg, nchini Afrika Kusini. Sehemu ya kwanza inaitwa \"Krokodil\" (Kiafrikaans kwa \"mamba\"). Baada ya kupokea mto wa Marico jina linabadilika na kuwa Limpopo. Hapo unapita mwendo wa upinde mkubwa ukielekea kwanza kaskazini-magharibi halafu mashariki hadi Bahari Hindi. unafuata mpaka kati ya Afrika Kusini na Botswana, halafu mpaka wa Afrika Kusini na Zimbabwe.",
"Milima ya Ufa Mashariki\nMilima ya Ufa Mashariki ni safu mbili za milima ya eneo la Maziwa makubwa ya Afrika, katika nchi a Kenya, Uganda, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Burundi.\nInaitwa hivyo kutokana na uhusiano wake na Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki; safu ya magharibi ina: Milima ya Virunga, Milima ya Mitumba na Milima ya Rwenzori, wakati ile ya mashariki ina vilele vya juu zaidi katika bara zima la Afrika: Mlima Kilimanjaro (mita 5,895, sawa na futi 19,340) na Mlima Kenya (mita 5,199, futi 17,058). Kati ya milima mingine kuna Mlima Elgon kati ya Kenya na Uganda. Yote, isipokuwa Ruwenzori ina asili ya volkeno.",
"Kaskazini-Magharibi (jimbo la Afrika Kusini)\nMji mkubwa ni Mafeking iliyounganishwa na Mmabatho (awali mji mkuu wa Bophuthatswana). Miji mingine yenye maana ni Potchefstroom, Klerksdorp, Brits, Rustenburg, Lichtenburg na Vryburg.",
"Johannesburg\nJapokuwa johannesburg ni mji mkubwa lakini sio miongoni mwa miji mikuu mitatu ya Afrika Kusini lakini mahakama ya katiba inakaa hapa.",
"Mkimbizi\nMnamo mwaka wa 2008 na 2009, hali ya kibinadamu ya kuhama kwa idadi kubwa ya Wazimbabwe, wakiingia nchi jirani ya Afrika Kusini, kulifanya tofauti kati ya \"wakimbizi\" na wa \"wahamiaji wa kiuchumi\" kufifia. Watu kama hao hawaambatani na jamii yoyote kikamilifu na wana mahitaji ya kijumla, haki na majukumu, yanayopatikana nje ya majukumu ya Ubalozi wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi. Wao huanguka kati ya nyufa, kulingana na ripoti iitwayo Uhamiaji wa Kizimbabwe Kuingia Afrika Kusini: Mielekeo Mipya na Majibu, iliyozinduliwa mnamo Novemba 2009 na Mpango wa Masomo ya Uhamiaji wa Lazima (FMSP kwa Kiingereza) katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Afrika Kusini. Kulingana na watafiti, ukosefu wa ulinzi wa wahamiaji katika kanda kulisababishwa na \"\"tofauti isiyo ya kweli\"\" kati ya kuwa mhamiaji wa kulazimishwa na mhamiaji wa kiuchumi. Ripoti hiyo ilipendekeza kuwa maneno bora zaidi yangekuwa \"wahamiaji wa kulazimishwa wa kibinadamu\", ambao wanahama kwa kusudi la kuishi kwao na kuishi kwa wanaowategemea."
] | 17
|
Je,yesu alikuwa na wafuasi wanawake?
|
[
"Salome (mke wa Zebedayo)\nSalome (kwa Kiebrania: שלומית, \"Shelomit\", kutoka mzizi שָׁלוֹם, shalom, yaani amani) alikuwa mke wa Zebedayo na mfuasi wa Yesu Kristo pamoja na wanae Yakobo Mkubwa na Mtume Yohane, waliokuwa marafiki wakuu wa Yesu pamoja na mtume Petro."
] |
[
"Yohane Mbatizaji\nBado mtoto alikwenda kuishi jangwani, labda kutokana na kifo cha wazazi. Wataalamu mbalimbali wanadhani kwamba huko alikuwa akiishi kati ya Waeseni, wafuasi wa madhehebu ya Kiyahudi yenye msimamo mkali hata kuliko ule wa Mafarisayo.",
"Yesu kadiri ya historia\nKwa ujumla zinathibitisha ya kwamba Yesu alikuwepo, na kwamba wakati hao walipoandika alikuwa na wafuasi huko Roma na ya kwamba awali Waroma hawakuelewa tofauti kati ya wafuasi wake na Wayahudi",
"Yesu\nNje ya Ukristo kuna habari fupi kuhusu Yesu katika maandiko ya waandishi wa Roma, Wagiriki na Wayahudi. Habari hizo zinaangaliwa sana kwa sababu zimetungwa na watu wasiomwamini Yesu kidini. Kwa ujumla zinathibitisha ya kwamba Yesu alikuwepo, na kwamba wakati hao walipoandika alikuwa na wafuasi huko Roma na ya kwamba awali Waroma hawakuelewa tofauti kati ya wafuasi wake na Wayahudi.",
"Kupaa Bwana\nUtawala wa Yesu umeanza hasa katika Kanisa lake linalokusanya wale waliomuamini kuwa ni Bwana wakaokolewa. Mungu “alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake” (Kol 1:13). Yesu alisema, “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu… Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu” (Yoh 18:36,37). “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza” (Lk 17:20). “Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia” (Math 13:33). Baada ya kufufuka, aliwajibu Mitume waliomuuliza kuhusu wakati wa kurudisha ufalme: “Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi” (Mdo 1:7-8).",
"Jinsia\nKwa msingi huo unaweza ukaeleweka uamuzi wa Yesu wa kuteua wanaume tu kuwa mitume ingawa aliwaheshimu sana wanawake, kuanzia Mama yake, Bikira Maria. Huyo, aliye kielelezo cha wanawake wote, kwa upendo wake kamili alichangia na anazidi kuchangia ustawi wa Kanisa na wa ulimwengu kuliko mtume yeyote yule. Kwa kuwa Yesu ametuonyesha kuwa jambo bora si kutawala, bali kupenda na kutumikia kama mwenyewe alivyofanya akiongozwa na Roho Mtakatifu, ambaye ndani ya Mungu ni Upendo-Nafsi, ni Zawadi-Nafsi anayekamilisha umoja wa Baba na Mwana. Ndiyo sababu anatusukuma kupenda na kujitoa badala ya kutaka kutawala. Katika hilo wanawake wanaelekea zaidi.",
"Yosefu Barsaba\nYosefu Barsaba (pia Yusto, yaani \"Mwadilifu\") alikuwa mmojawapo kati ya wafuasi wa kwanza wa Yesu.",
"Kristo Mfalme\nUtawala wa Yesu umeanza hasa katika Kanisa lake linalokusanya wale waliomuamini kuwa ni Bwana wakaokolewa. Mungu “alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake” (Kol 1:13). Yesu alisema, “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu… Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu” (Yoh 18:36,37). “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza” (Lk 17:20). “Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia” (Math 13:33). Baada ya kufufuka, aliwajibu Mitume waliomuuliza kuhusu wakati wa kurudisha ufalme: “Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi” (Mdo 1:7-8).",
"Yohane Mbatizaji\nYohane alikuwa pia na kundi la wafuasi walioendelea kama ushirika baada ya kifo chake.",
"Makabila ya Israeli\nKama kawaida ya mitara, kulikuwa na upendeleo na wivu. Hasa Yosefu alichukiwa na kaka zake wote, ingawa alikuwa mnyofu hata kuwasimulia ndoto zake za ajabu (Mwa 37:2-11). Kijicho na chuki vilifikia hatua ya kuwafanya watamani kumuua. Walipopata nafasi walifanya njama, ingawa si wote. Mwisho uamuzi ukawa kumuacha hai lakini kumuuza kama mtumwa kwa wafanyabiashara walioelekea Misri (Mwa 37:12-36). Lakini katika maovu ya binadamu Mungu akazidi kushughulikia taifa lake teule. Hivyo Yosefu akawa mfano wa Yesu ambaye alichukiwa bure tu akauawa msalabani kwa wokovu wa wadogo zake wakosefu.",
"Jinsia\nKimsingi zaidi, inafaa tujitahidi kuelewa fumbo la Mwana wa Mungu kujifanya mwanamume awe bwanaarusi wa Kanisa linalokusudiwa kumzalia watu wote kabisa. Ingawa Mungu hana mwili, na kwa sababu hiyo hana jinsia, Yesu Mwanae ni mwanamume na ametushirikisha uhusiano wake na Mzazi wa milele aliyemuita Baba. Hilo si bure: ndiye aliyetangulia kutupenda na ndiye anayetuwezesha kufanya lolote. Kazi yetu ni hasa kuwa tayari kupokea upendo wake na utendaji wake wowote ili uzima ustawi ndani mwetu na kandokando yetu."
] | 21
|
Je, mji mkuu wa Jibuti ni upi?
|
[
"Jibuti (mji)\nMsafiri mmoja mwandishi alielezea mji Jibuti kama mji ulio na shida ya kujitambulisha, alisema ya kwamba \"mji wa kudumu kwa taifa la wahamiaji, ni mji wa Kiafrika uliotengenezwa kama makao ya Kiulaya na pia kama Hong Kong wa Kifaransa kwa Bahari ya Shamu.\"",
"Jibuti (mji)\nHulka za mji wa Jibuti ni mapwa kwa pwani ya magharibi na soko kubwa la kati, na uwanja wa michezo wa taifa, Jumba la Rais na Msikiti Hamouli.",
"Jibuti (mji)\nJibuti (kwa Kiarabu جيبوتي) ni mji mkuu na mji mkubwa nchini Jibuti ukiwa na wakazi 400,000.",
"Jibuti\nJina la nchi linatokana na lile la mji mkuu, Jibuti."
] |
[
"Kismayu\nKismayu (pia: Kismayo au (Kisomali: Kismaayo) ni mji katika mkoa wa Jubbada Hoose wa Somalia mwambaoni wa Bahari Hindi. Uko karibu na mdomo wa mto wa Juba. Kismayu ndio mji mkubwa katika eneo la Jubbaland. Mji wenyewe uko 528km kusini magharibi mwa mji mkuu Mogadishu. Katika mwaka wa 2011, Kismayu ilikadiriwa kuwa na wakaazi 183,300.",
"Toyota, Aichi\nMji wa Koromo (挙母市), ulilotangulia Toyota, ulikuwa maarufu kwa utayarishaji kuu ya hariri na akafanikiwa katika kanda Mikawa kutoka Meiji Era kupitia kipindi Taishō. Baada ya mahitaji ya hariri malighafi kupungua katika Ujapani na nje ya nchi, mji ullianza kushuka. Kushuka huku kulimtia moyo Kiichiro Toyoda, binamu yake Eiji Toyoda, ili kutafuta njia mbadala ya biashara ya familia ya viwanda vya gari. Utafutaji uliongoza katika uwanzilishi wa Kampuni ya Toyota ya Magari.\nMji huu ulipata hadhi ya mji tarehe 1 Machi, mwaka wa 1951. Mji huu ulibadilishs jina lake kuwa Toyota mwaka wa 1959, na mwaka mmoja baadaye, ukawa mji dada wa mji wa magari mwingine, Detroit, Michigan. Toyota-shi ni mapacha pia na eneo la Derbyshire, Uingereza, ambapo Toyota huwa kama kituo cha uundaji.\nTarehe 25 Machi,mwaka wa 2005, Expo 2005 ilifunguliwa na makao yake makuu katika Nagakute na shughuli za ziada katika Seto na Toyota. Expo iliendelea hadi 25 Septemba 2005.",
"Utsunomiya, Tochigi\nUtsunomiya (宇都宮市) ndiyo mji mkuu katika mkoa wa Tochigi. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2010, mji una wakazi wapatao 510,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 105 kutoka juu ya usawa wa bahari. Eneo lake ni 416.84 km².",
"Uwanja wa Keitaba\nUwanja wa Keitaba ni uwanja mkuu wa mpira wa miguu katika Wilaya ya Bukoba Mjini mkoani Kagera.",
"Jibuti (mji)\nMji huo ulianzishwa na Ufaransa kama bandari mwaka wa 1888, ukawa mji mkuu mwaka wa 1891, ukiandamwa na Tadjourah.",
"Yaita, Tochigi\nYaita (矢板市, \"Yaita-shi\") ni mji wa Japani katika mkoa wa Tochigi. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2010, mji una wakazi wapatao 35,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 190 kutoka juu ya usawa wa bahari. Eneo lake ni 170.66 km²."
] | 26
|
Je,Mengistu Haile Mariam alizaliwa lini?
|
[
"Mengistu Haile Mariam\nMengistu alizaliwa tar. 27 Mei 1937 katika mji wa Addis Ababa. Babake Haile Mariam alikuwa mtumishi wa mkabaila na gavana wa sehemu ya jimbo la Shoa. Wazazi wake walitoka katika kusini ya Ethiopia (leo: Jimbo la Mataifa ya Kusini). Mamake Mengistu alikufa alipokuwa mdogo wa miaka 8 kwa hiyo aliishi kwa bibi yake pamoja na wadogo zake. Baadaye akarudi akaishi pamoja na babake na kuingia jeshini. Alipanda ngazi ya vyeo hadi kuwa meja.",
"Mengistu Haile Mariam\nMengistu Haile Mariam (Amhaars: ሊየተና ኮሎኔል መንግስቱ ኃይለ ማርያም), *21 Mei 1937), ni mwanajeshi na mwanasiasa kutoka nchi ya Ethiopia aliyewahi kuwa rais wa Ethiopia hadi kupinduliwa mwaka 1991."
] |
[
"Haile Mariam Desalegne\nHaile Mariam alizaliwa mwaka 1965 katika wilaya ya Boloso Sore kwenye kanda la Wolayita lililopo katika kusini ya Ethiopia. Familia yake ni sehemu ya kundi la Wawolayta na wakristo; tofauti na asilimia kubwa ya Wawolayta Haile Mariam anafuata aina ya ukristo wa kipentekoste katika kanisa la Hawariyat (Kanisa la kimitume la Ethiopia)",
"Mengistu Haile Mariam\nMengistu alitumwa Addis Ababa kama mwakilishi wa kikosi chake. Katika majadiliano ya kamati aliweza kujipatia nafasi muhimu akachaguliwa kuwa makamu wa mwenyekiti. Chini ya uongozi wake mtawala Haile Selassie alikamatwa na kufungwa ndani nadi kifo chake mwaka uliofuata 1975. \nMengistu aliendelea kishika madaraka akahakikisha kuuawa kwa majenerali wa jeshi la Haile Selassie na pia maafisa kadhaa waliompinga ndani ya Derg.\nTangu mwaka 1977 Mengistu aliweza kuua wapinzani wake wote ndani ya jeshi na Derg akatangaziwa kuwa mkuu wa dola.",
"Mengistu Haile Mariam\nChama cha wafanyakazi wa Ethiopia kilianzishwa mwaka 1984 kikiwa chama cha pekee kilichoongozwa na kamati kuu. Mengistu alikuwa mwenyekiti wa chama na pia rais wa nchi tangu 10 Septemba 1987. Jina la nchi lilibadilishwa kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Ethiopia.",
"Haile Mariam Desalegne\nHaile Mariam Desalegne (* 19 Julai 1965 Boloso Sore, Wolayita, Ethiopia) ni mwanasiasa wa nchini Ethiopia. Mwaka 2010 alikuwa waziri wa mambo ya nje na makamu wa waziri mkuu wa Ethiopia. Baada ya kifo cha waziri mkuu Meles Zenawi terehe 20 Agosti 2012 alikuwa waziri mkuu mtendaji.",
"Mengistu Haile Mariam\nMwaka 1974 serikali ya kaisari Haile Selassi ilishindwa kutatua matatizo ya ukame, njaa na mvurugo wa wananchi waliosikitika serikali. Sehemu za jeshi zilianza kukataa utekelezaji wa amri. Kamati ya maafisa wa ngazi iliundwa Addis Ababa kwa shabaha ya kurudisha utaratibu nchini. Baada ya miezi ya kwanza walipanusha kamati yao kwa wawakilishi kutoka kila kikosi cha jeshi na kamati ilijulikana kwa kifupi chake cha \"Derg\".",
"Mengistu Haile Mariam\nJeshi la Mengistu ilipata misaada mingi kutoka Umoja wa Kisovyeti na nchi nyingine za kikomunisti hasa Ujerumani ya Mashariki. Hata hivyo wakati harakati ya ukombozi wa Tigray ilipoungana na vikundi kutoka majimbo mengine na kuunda umoja wa EPRDF muundo wa ukomunisti ulianza kuporomoka katika nchi za Ulaya na msaada kwa Mengistu kutoka kule ulipungua.",
"Haile Mariam Desalegne\nHaile Mariam hakushiriki katika shughuli za mapinduzi yaliyopindua udikteta wa kikomunisti wa Mengistu mwaka 1991 maana wakati ule alikuwa masomoni huko Ufini. Lakini baada ya ya kujiunga na EPRDF aliteuliwa mwaka 2000 kuwa makamu wa rais la jimbo la Mataifa ya Kusini na tangu mwaka 2001 hadi 2006 pia raisi yake.",
"Mengistu Haile Mariam\nKwa kufuata mfano wa Umoja wa Kisovyeti serikali ililenga kusimamia matawi yote ya uchumi na kupanga uzaaji wa mavuno na bidhaa. Ardhi yote pamoja na makampuni makubwa ya kibiashara yalitaifishwa; wakulima waliwekwa huru na mabwana wao wa awali lakini wakalazimishwa kufanya kazi katika vijiji vya pamoja hawakupewa ardhi ya binafsi.",
"Mengistu Haile Mariam\nKatika ipindi cha miaka ya 1980 serikali ya Mengistu iliona matatizo mengi. Sehemu za sababu zilikuwa kimazingira kama ukame; mengine kisiasa kwa sababu mabadiliko ya uchumi yalileta uhaba wa mazao na vifaa. Kutokana na mipango ya uchumi kilimo kilikwama kabisa kwenye mikoa kadhaa. Njaa kubwa ilitokea 1984-1985 iliyokuwa vibaya zaidi kuliko ile ya zamani za Kaisari Haile Selassie. Watu walianza kupinga serikali na uchukua silaha katika sehemu mbalimbali za nchi."
] | 44
|
Je,nani aligundua kifaa cha darubini?
|
[
"Darubini\nDarubini (kutoka Kiajemi: دوربين, \"dorbin\") ni kifaa cha kutazamia vitu ambavyo viko mbali. Kutegemeana na kusudi lake kuna aina mbalimbali:Darubini ya kwanza inayojulikana ilitengenezwa mwaka 1608 na Mholanzi Hans Lipperhey aliyekuwa fundi miwani akaunganisha lenzi mbili katika bomba."
] |
[
"Chocheeni Kuni\nUBETI WA KWANZA:\nWatanzania, mwenda kwao siku zote haogopi giza\nAcheni nirudi nyumbani safari imenishinda, nauli zenu nitarudisha.\nMtu anatapika nyongo yake, anailamba tena anaangaliwa\nNi sawa na tawi kavu linapoanguka watu wakapiga kelele, ayaaaa\nKatika misimu minne kwa mwaka, tuongeze msimu mwingine wa kujiridhisha\nRaha ya jamvi siku zote ni viraka viraka,\nNa dungu, linamficha mlinzi wa ndege wakati wa mvua tu\nEti ooo, imenyesha juzi tu, maji sio mengi, nisubirini kule\nIlishindikana vipi kuyapima maji kwa mti, ndio mkawaambia watu wavuke\nMjomba, binadamu ni kama ganda la kitabu,\nMpaka umfungue maandishi, ndio uweze kumuelewa\nEti lilotokea mbali tufanye limepita, na haliwezi kumdhuru mwingine\nKweli! Inayotaka kunyesha huwa haisubiri mawingu\nMimi, sidhani kama kujiponya kwa mambo mazito\nTunahitaji cheti kilichogongwa muhuri wa moto\nAu mtaalamu wa magonjwa ya akili, zaidi ya kutumia neno sahau tu\nUnawaulizaje watu magongo ya nini, wakati umesema kuna nyoka?\nMjomba, wewe si uliwapaka wanja, ngoja wao wakupake pilipili\nHalafu kwenye kombolela iwe zamu yako kuzinga",
"Nabii Eliya\nHapo Mungu akamtuma Eliya wa Tishbi (1Fal 17-18) ambaye jina lake lina maana ya kwamba, “Mungu wangu ni YHWH” na linajumlisha kazi yake ya kutetea kwa ari zote imani ya kweli hata akaiokoa. Ili kuondoa utata wa kuabudu pande mbili, Eliya kwanza alizuia mvua isinyeshe nchini miaka mitatu na nusu, ibada kwa Baali zisifanikiwe hata kidogo, halafu akashindana na manabii hao hadhara ya Israeli yote juu ya mlima Karmeli. Tofauti na mbinu za manabii 450 wa Baali, waliofikia kujichanja na kutoka damu ili kuvuta moto kutoka mbinguni wasifaulu, Eliya aliomba tu kwa unyofu kwamba Mungu ajitokeze ili kugeuza mioyo ya watu wake wamrudie. Kwa kuteremsha moto toka mbinguni juu ya sadaka yake YHWH alithibitisha kuwa ndiye Mungu pekee na kuwa anaendelea kuwaokoa watu wake. Baada ya Eliya kuwachinja wote aliruhusu mvua inyeshe tena. Ndiyo sababu anasifika kwa nguvu ya sala yake (Yak 5:17-18).",
"Duma (Siri ya Mtungi)\nMara kadhaa ameonekana kujutia nafsi yake kwa kujihusisha na shughuli za kitapeli na mali za magendo na mihadarati, lakini shida na hanasa za maisha zinamfanya akose misimamo thabiti na kuendelea upande wa pili. Aliweza kumwambia Masharubu hataki mali zake za magendo, lakini alishindwa kumkatalia Golden na Ish mipango yao ya uingizwaji wa dawa za kulevya mjini Bagamoyo na kuzileta eneo la Dar es Salaam. Duma ana mahusiano ya kimapenzi ya dhati na Nusura, lakini vilevile ana mahusiano na wanawake wengine kibao huko vilabuni. Vilevile aliwahi kuishi kinyumba na Rose mwishowe akamwingiza mjini kwa kumlengesha kwa maaskari na kumwacha akiwa apeche alolo. Sifa kubwa ya Duma ni kutokubali kushindwa na mapenzi ya hali ya juu kwa mdogo wake Steven.",
"Historia ya Wokovu\nMatendo mengine tofauti yaliyoathiri sana maisha ya Daudi ni dhambi alizotenda kwa ajili ya mke wa Uria Mhiti, yaani uzinifu, unafiki, ulevyaji na uuaji wa askari huyo mwadilifu (2Sam 11). Basi, Nathani akamuendea ili kumlaumu na kumtabiria adhabu mbalimbali, hasa kwamba upanga hautaondoka nyumbani kwake (2Sam 12:1-25). Ikawa hivyo hasa kwa sababu ya Absalomu mwanae ambaye alimuua kaka yake (2Sam 13:22-37) na baada ya kusamehewa akafanya njama hata akamfukuza Daudi toka Yerusalemu (2Sam 14:28-15:29) akazini na masuria wake mahali pa wazi (2Sam 16:20-23). Hata hivyo Daudi akazidi kumpenda na alipoambiwa amekufa akamlilia kwa namna ambayo iliwashangaza na kuwachukiza waliompigania: yeye ambaye alijiombea na kupewa msamaha wa Mungu hakumchukia mwanae aliyehatarisha maisha yake (2Sam 18:19-20:8).",
"Isa\nNabii Isa aliletwa kwa wanadamu kufikisha ujumbe kwao wa kuwafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mmoja, hana mwenzake, na kuwa Yeye pekee ndiye mwenye kustahili kuabudiwa kwa haki. Ujumbe huu ndio ujumbe uleule uliotumwa kwa Mitume na Manabii wote kwa wanadamu ili kuwaongoza, naye alikuja kutilia mkazo na kusisitiza jambo hili na kuzipa nguvu tume za Mitume na Manabii waliopita.",
"Leonardo da Vinci\nWakati Leonardo ameshakua, aliandika vitu viwili tu kuhusu maisha yake ya utotoni. Alikumbuka kwamba alivyokuwa amelala kwenye kitanda chake cha watoto nje ya nyumba yao ndege mkubwa alikuwa akipaa na kumzungukazunguka juu yake. Mikia yake ikawa inamfutafuta sura yake. Kumbukumbu nyingine muhimu ya Leonardo ilikuwa vipi aligundua pango milimani wakati anapeleleza. Alikuwa na hofu kubwa sana huenda kukawa na kiumbe kikubwa cha ajabu kimejificha mle ndani ya pango. Lakini pia alikuwa na hamu na shauku ya kujua kilichopo mle ndani.",
"Nabii Isaya\nKatika kutuliza watu alimtabiria mfalme Ahazi kwamba mwanamwali atamzaa mtoto wa kiume atakayethibitisha uwepo wa Mungu pamoja na watu wake, jina lake Emanueli linavyomaanisha. (7:1-17) Kweli mke wa Ahazi alimzaa Hezekia atakayeendeleza ufalme wa ukoo wa Daudi, lakini utabiri huo ulimlenga zaidi Yesu, mwana wa Bikira (walivyoelewa watafsiri wa kwanza wa Biblia katika Kigiriki) ambaye kweli ni Mungu pamoja nasi, na ni mwana wa Daudi ambaye atatawala milele kwa amani na haki (11:1-9).",
"Neema Decoras\nKatika studio hiyo alifanikiwa kurekodi na kutoa albamu yake ya kwanza mwezi Julai mwaka wa 2013. Albamu hiyo iitwayo “Milele Nitalisifu Jina Lako” ina nyimbo nane ambazo zote ameziimba kwa lugha ya Kiswahili. Nyimbo zilizomo katika albamu hiyo ni; Milele Nitalisifu Jina Lako, Mikononi mwa Mungu, Unapojaribiwa, Nione Leo, Mungu ni Mwema, Rejea kwa Yesu, Ninaimba Sifa na Hakika Nimejua.\nAkiongozwa na Neno kutoka katika Zaburi 145:1-2 “Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi Jina lako milele na milele. Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu Jina Lako Milele na Milele” Neema Decoras anasema kamwe hawezi kuacha kulisifu Jina la Bwana kwa kuwa Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana.",
"David James Thouless\nDavid James Thouless (amezaliwa 21 Septemba, 1934) ni mwanafizikia kutoka nchi ya Uingereza. Hasa aligundua m . Mwaka wa 2016, pamoja na Frederick Duncan Michael Haldane na John Michael Kosterlitz, alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Alipewa tuzo kwa utafiti wake wa kinadharia katika maelezo ya tabia za mata katika hali karibu na sifuri halisi (ing. \"\"for theoretical discoveries of topological phase transitions and topological phases of matter\"\")\nProfesa John Chalker, mkuu wa idara ya Fizikia ya Kinadharia kwenye Chuo Kikuu cha Oxford anajaribu kueleza tuzo ya Nobel ya 2016 kwa maneno ya kiraia",
"Kupashwa habari\n26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, 27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. 28 Malaika akamwendea, akamwambia, \"Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.\" 29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini? 30 Malaika akamwambia, \"Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. 31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu. 32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake. 33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.\" 34 Maria akamjibu, \"Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?\" 35 Malaika akamjibu, \"Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu. 36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa. 37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.\" 38 Maria akasema, \"Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.\" Kisha yule malaika akaenda zake.",
"Galileo Galilei\nGalileo Galilei (5 Februari 1564 – 8 Januari 1642) alikuwa mtaalamu wa fizikia, hisabati na astronomia kutoka nchini Italia."
] | 24
|
Je somo la kiswahili linafunzwa Uganda?
|
[
"Mwajuma Selemani Mohamed\nHARAKATI ZAKE ZA UANDISHI.\nMwajuma alianza kujishughulisha na uandishi wa Riwaya na Ushairi tangu alipokuwa anasoma sekondari. \nKipaji hicho alikiendeleza hata alipokuwa Chuoni. \nBaada ya jitihada kubwa sana alizozionyesha chuoni kama mdau mkubwa wa kiswahili hatimae alijiunga na CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU VYA AFRIKA YA MASHARIKI (CHAWAKAMA) na kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti, na baade muweka hazina, katika kitivo cha Elimu Chuo Kikuu cha Dodoma. \nMwandishi huyu hakuishia hapo katika kuipigania lugha hii adhimu ya kiswahili kwani aliamua kujiunga na CHALUFAKITA na mwaka 2017 alipata tuzo ya mwalimu mbunifu wa somo la kiswahili. \nMpaka sasa ni mjumbe wa CHAMA CHA LUGHA NA FASIHI YA KISWAHILI TANZANIA (CHALUFAKITA) kanda ya kaskazini.\nSio hivyo tu bali ni Mwenyekiti wa CHAWAVITA) Chama cha Waandishi wa Vitabu Tanzania .\nhadi sasa Mwajuma amefanikiwa kutoa kitabu kimoja kiitwacho NDOA YA USALITI\nPamoja na kwamba hiki ndicho kitabu chake cha kwanza kukichapisha lakini mwandishi huyu anamiswada mingine ambayo yuko mbioni kuichapisha kama vile:",
"Kiswahili\nKuna taasisi zinazolenga kukuza na kuimarisha Kiswahili kama vile Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na idara za Kiswahili katika vyuo vikuu vingine vya Kenya na pia Uganda."
] |
[
"Gideon Byamugisha\n1992 alipokea baraka ngazi ya ukasisi akapewa jukumu la kufundisha chuo cha theolojia Mukono (sasa: Chuo Kikuu cha Kikristo cha Uganda). Wakati ule alifuata ushauri kutafuta upimaji wa damu yake ahakikishe hana UKIMWI. Alipopimwa akaonekana kuwa na viini vya HIV vilevile. Aliambiwa matokeo dakika chache tu kabla ya kuwa na somo chuoni. Aliamua kuwaambia wasikilizaji wake wakiwa na walimu wenzake ya kuwa amepatikana na HIV.",
"Muhammed Said Abdulla\nNje ya riwaya za upelelezi aliandika pia Mke Mmoja Waume Watatu (1975) kinachohusu ulaghai katika ndoa na mkusanyo wa hadithi fupi katika \"Hekaya za Kuburudisha\". \nAbdulla alikuwa ni mhariri na mwaandishi wa vitabu tofauti ambavyo viliinyanyua lugha ya kiswahili katika daraja la juu na kuiongezea umaarufu mkubwa eneo la afrika mashariki. Alifanikiwa kuowa mke na kupata wawili katika maisha yake. Vile vile ni miongoni mwa watetezi wakubwa walifanya utetezi katika kuikomboa nchi ya Zanzibar kutoka mikononi mwa Watanganyika. Na hii ndio ilikuwa sababu ya yeye kuwa katika hatari ya maisha yake. Miongoni mwa beti zake za kuwatupia watanganyika ujumbe utakaoweza kuwapotezea nguvu ya kutaka kuinyakuwa Zanzibar. Njama ilianza kupangwa na watanganyika ili kumuondoa Bwana Msa Katika hii dunia. Aliuwawa yeye na familia yake, mkewe na watoto wake wawili wa kike katika kipindi cha mapinduzi ya Zanzibar. Hili lilikuwa pigo kubwa sana kwa Wazanzibari wote kwa kuuwawa Bwana Msa katika mazingira ya kutatanisha.",
"Historia ya Kiswahili\nWaingereza baada ya kuchukua Tanganyika kutoka kwa Wajerumani waliendela kutumia Kiswahili kama lugha ya utawala. Kuanzia mwaka 1930 waliunda kamati yenye shabaha ya kuunganisha lahaja mbalimbali na kuunda Kiswahili cha pamoja kwa ajili ya Afrika ya Mashariki (Inter-territorial Language (Swahili) committee for the East African Dependencies). Mwenyekiti alikuwa Frederick Johnson, makatibu R. K. Watts, P. Mzaba na Seyyid Majid Khalid Barghash. Kamati hiyo iliamua kutumia lahaja ya Kiunguja kuwa msingi wa Kiswahili cha pamoja kilichoendela kufundishwa shuleni. Leo hii ni Kiswahili rasmi kinachofunzwa na wanafunzi na kuandikwa magazetini na vitabuni.",
"Kanku Kelly\nAkiwa shule ya msingi walifundishwa somo la muziki na yeye alikuwa akifanya vizuri sana na kuwa mmoja kati ya wanafunzi bora wa somo hilo. Akifafanaua juu ya kufukuzwa shule, Kelly anasema “Nilikuwa anapenda muziki kupita kiasi, nikiwa darasani mwalimu alinikuta nikiandika wimbo wa ‘Amba’ uliotungwa na Nyboma Mwandido ndipo nikafukuzwa shule”. Kanku anasema baada ya kufukuzwa shule mwaka 1974, alihitajika kujiunga na jeshi la nchi hiyo katika kitengo cha muziki wa Brass band, lakini akakataa akiwa na dhamira kubwa kuwa mwanamuziki mashuhuri. Anaeleza kuwa jamaa zake aliokuwa nao darasani asilimia tisini walipelekwa jeshini kupiga muziki wa Brass band.",
"Wasangu (Tanzania)\nSasa kuku mweusi hutafutwa (sehemu zingine mbuzi au kondoo hutafutwa kwaajili ya shughuli hizi). Mambo yote yakiwa tayari watu wote wanaohusika hjuenda mahali palipo patakatifu na kuanza kuomba mvua inyeshe. Kasisi mkuu huanza kusema maneno haya. \"Uposhele inguku ini tuhanzaje hwunzi hwilwipei invula itonye, iviyabo vihwone. Ingukuinj mulyarrje mwendi mwikwizyanajei abantu balalamiha baiga, \"Tukosile yenu? Invulayinyu Mhutima?\"Tulaba twalamba sana ngatukosile shimo vyanje. Ngazilipo zimo uvitilwe utuwozye we wewe dada pipo nahumo uhwinyi washimbilile. Tusubila wenewe ungulubi uwinji numo.\"",
"Alice Lakwena\nAlice Lakwena, pia: Alice Auma (1956 - 17 Januari 2007) alikuwa kiongozi wa kiroho kati ya Waacholi wa Uganda aliyeanzisha kundi la \"Harakati ya Roho Mtakatifu\" (Holy Spirit Movement) na kuendesha vita ya msituni dhidi ya serikali ya rais Yoweri Museveni kuanzia Agosti 1986 hadi Novemba 1987.",
"Wikipedia ya Kiswahili\nKumbe mnamo Juni 2018, Wikipedia ya Kiswahili imekuwa inafunguliwa na 0,009% ya wanaofungua Wikipedia duniani kote. Walioivinjari mwezi huo walikuwa katika nchi zifuatazo: Tanzania 37.9%, Marekani 30.3%, Kenya 18.0%, Ufaransa 3.8%, Ufalme wa Muungano 3.3%, kwingineko 6.7%.",
"Haki za binadamu nchini Uganda\nWakala wa usalama wa Uganda wamekuwa wakihusishwa na mateso ya haramu na ufungo haramu wa washukiwa, pamoja na waasi wa LRA na wateteaji wao. Mbinu za utesaji ni kama kuwafunga washukiwa kwa mbinu ya 'kandoya' (mikono na miguu hufungwa nyume ya mheshimiwa) kutumia kamba kutoka dari, kali na kumpiga mateke, na kushikisha waya za stima katika sehemu zake nyeti.",
"Historia ya Kiswahili\nUganda inatumia Kiswahili kama lugha ya polisi na jeshi, hali ambayo haikuongeza upendo wa Waganda kwa lugha kutokana na historia ya Uganda ya kuwa na vita na serikali za kijeshi. Lakini kinasikika pia kama lugha ya biashara masokoni. Pamoja na kwamba Waganda walikichukulia Kiswahili kama lugha ya kitumwa lakini pia lugha hii ilionekana kuwa na ustaarabu wa Kiarabu zaidi, yaani Uislamu. Lugha ya Kiswahili ilitumika katika kueneza dini hiyo."
] | 57
|
Simone Gooden alizaliwa wapi?
|
[
"Monie Love\nSimone Gooden (amezaliwa tar. 2 Julai 1970), anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Monie Love, ni emcee kutoka nchini Uingereza na mtangazaji wa redio wa zamani huko nchini Marekani. Alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika hip hop ya Kiingereza, na kuleta mgongano/athira kubwa na wasaili/maemcee wengine wa kike wa Kimarekani kama vile Queen Latifah, vilevile kupitia uanchama wake na baadhi ya makundi mwishoni mwa miaka ya 1980/mwanzoni mwa miaka ya 1990 - Native Tongues. Love alikuwa miongoni mwa wasanii wa kwanza wa BritHop kuingia mkataba na kusambaziwa kazi zake dunia nzima na mastudio makubwakubwa duniani.",
"Monie Love\nLove alizaliwa katika eneo la Battersea la mjini London. Huyu ni mdogo wake mwnamuziki wa muziki wa techno Dave Angel, na alikuwa binti wa baba aliyekuwa akipiga muziki wa jazz kutoka mjini London."
] |
[
"Simone Deveaux\nKwenye kipengele cha \"One Giant Leap\", Simone anachukua mchoro wa Claire na Zach na kumweleza Isaac kwamba anaenda kuziuza picha zile na kisha aende kufanyiwa uondolewaji wa matumizi mabaya ya dawa za kulevya. Wakati Isaac anakataa, akaachana naye. Siku ile baadaye, Peter Petrelli, ambaye hivi karibuni amekuwa akimwuguza baba wa Simone, amekiri penzi lake kwa Simone. Ijapokuwa wawili hao walitumia pamoja usiku wao, lakini bado Simone hataki kuwa na pupa ya mahusiano mapya.",
"Genesis (Heroes)\nIsaac Mendez ni msanii na mtawaliwa wa heroin aishiye mjini New York City. Anadai ya kwamba anaweza kuchora picha zenye kuonesha matukio ya baadaye, lakini mwanamke wake, Simone Deveaux, lakini mama anaamini ni athari za dawa za kulevya tu zinamfanya awe vile. Baadaye, kufuatia kujikita dawa kadhaa za kulevya, kachora mfano wa mlupuko wa bomu nyuklia linaangamiza mji wa Manhattan. Niki Sanders, kahaba wa mtandaoni huko mjini Las Vegas, Nevada, anagundua nguvu zake wakati yeye na mtoto wake Micah wanalazimika kutoroka dhidi ya majambazi wanaonyemelea nyumba yao. Wakati wa kutoroka, Niki anaamini kwamba anaone akisi ambayo si yeye. Amemwacha Micah kwa rafiki yake na kurudi nyumbani, ambapo wale majambazi wakamdaka na kumlazimisha amwagie vimbwanga vya ukahaba wakati wao wanamtazama. Kipengele hiki anaonekana kuzilai wakatia anacheza, kuamka baadaye kakuta wale watu wameauwa kikatili na mtu asiyejulikana. Akisi yake ya ajabu inamwonesha anyamaze kimya. Wote wawili Isaac na Niki wanagundua nguvu zao kuwa \"si za kuzikaribisha hivyo basi lazima wanashughulikie na waondokane nazo.\"",
"Simone Deveaux\nBaada ya ndugu wa Peter, Nathan, amezipata zile picha, yeye na Simone wakazifungua pamoja. Nathan akazichana-chana zile picha, kitendo ambacho kimemkera Simone. Hata hivyo, amekuwa na uwezo wa kumwonesha Peter nakala ya dijitali na picha imeonesha kuna mtu kafa lakini anafanana na Peter. Pamoja na hayo, Peter anaamua kwenye katika shule ya Union Wells na kwenda kumwokoa Homecoming aliyeonekana katika picha. Simone akaanza kuamini kwamba Isaac anaweza kuchora matukio ya baadaye, na kuamini kwamba Peter atarudi salama.",
"Simone Deveaux\nWakati Simone Deveaux anatambulishwa katika sehemu ya kwanza, yeye ni mwuza michoro anayeishi mjini New York City ambaye ana-mahusiano ya kimapenzi na msanii Isaac Mendez. Hata hivyo, lakini amekuwa akikerekwa sana uzoezi wa matumizi mabaya ya heroini yanayofanywa na Isaac na kujidai kwamba akitumia dawa hizo ndipo anakuwa na uwezo wa kuchora matukio ya baadaye.",
"Isaac Mendez\nHadithi ya Isaac Méndez inaanza katika sehemu ya kwanza, ambapo anajitafutia, na msanii mwenye mateso aishiye huko kwa tabu huko mjini New York City. Mpenzi na mnunuzi wake mkuu ni Simone Deveaux. Mendez ametawaliwa na heroini, na alifanikiwa kiasi kuacha matumizi haya mabaya kabisa, anaweka mkazo juu ya mahusiano yake na Simone. Mkazo huu umeharibika wakati Isaac anagundua kwamba anaweza kuona na kuchora matukio ya baadaye—lakini akiwa katika hali ya ulevi wa heroini tu. Hapo awali, Isaac anafikiri michoro ile kuwa ni \"ushetani\" na hata kujaribu kuziangamiza, lakini Simone anaziona kama ni mvuto wa kisaniii. Karibia na mwishoni mwa sehemu ya kwanza, Isaac anajidunga dawa kupita kiasi. Simone analeta msaada wa mwuguzi ambaye ni Peter Petrelli, ambaye anagundua kwamba Isaac amechora picha ya Peter bila hata ya kuonana naye hapo awali. Kwa msaada wa Peter, Isaac ananusurika katika kujikita dawa kupita kiasi.",
"Alyson Hannigan\nHannigan ameolewa na mwigizaji mwenzake wa katika tamthilia ya \"Buffy the Vampire Slayer\" Alexis Denisof katika hoteli ya Two Bunch Palms Resort huko mjini Desert Hot Springs, California, mnamo tar. 11 Oktoba, 2003. Wawili hao wana watoto wawili wa kike, Satyana Marie Denisof, amezaliwa mnamo tar. 24 Machi, 2009, na Keeva Jane Denisof, amezaliwa mnamo tar. 23 Mei, 2012.\nHannigan ni mama mlezi wa mtoto wa kiume wa Joss Whedon, Arden, na mume wake, Alexis Denisof, ni baba mlezi wake.",
"Sherone Simpson\nSherone Simpson (alizaliwa 12 Agosti 1984) ni mwanariadha wa nchi ya Jamaika ambaye huiwakilisha nchi yake katika mashindano ya kimataifa. Alishinda medali ya dhahabu katika mbio ya 4 x 100m katika mashindano ya Olimpiki ya 2004 na medali ya fedha katika Mashindano ya Mabingwa wa Dunia ya 2005.Alishinda medali ya fedha katika mbio ya 100m katika Olimpiki ya 2008 baada ya kukimbia kwa muda mmoja na mwenzake wa Jamaika ,Kerron Stewart. Muda wake wa kibinafsi wa 10.82 s katika mbio ya 100m,Simpson ndiye mwanariadha mwanamke wa nne bora nchini Jamaika.Mbele yake ni Merlene Ottey,Shelly-Ann Fraser na Kerron Stewart. Muda wake bora wa 22.00 s katika mbio ya 200m ndio muda wa nne bora katika orodha ya Jamaika akiwa nyuma ya Merlene Ottey,Grace Jacson,Juliet Cuthbert,Veronica Campbell-Brown na Kerron Stewart. Amekimbia mbio ya 200m na muda huu mara mbili. Kocha wa Simpson ni Stephen Francis mjini Kingston.Jamaika, anaposoma katika Chuo Kikuu cha Teknolojia. Yeye ,pia, alisoma katika shule ya Manchester High.\nSimpson alishinda medali ya dhahabu katika mbio ya wanawake ya 200 m katika Michezo ya Jumuia ya Madola ya 2006 , huku akishinda Veronica Campbell.Katika mbio hizo, Jamaika ilishinda medali za dhahabu kwa mbio za 100m na 200m. Jamaika ilishinda ,pia, medali zote za dhahabu katika mbio za kuruka viunzi.",
"Laurence Fishburne\nFishburne amemwoa Hajna Moss mnamo mwaka 1985, nchini Ethiopia. Kwa pamoja wakazaa watoto wawili: wakiume, Langston, aliz. 1987, na wakike, Montana, aliz. mnamo 1991. Fishburne na Moss wakajakutarikiana kunako miaka ya 1990. Mke wa sasa wa Fishburne ni mwigizaji mwenzake filamu bi. Gina Torres, ambaye walioana mnamo tarehe 20 ya mwezi wa Septemba mwaka wa 2002. Kwa pamoja wana mtoto mmoja wa kike aitwaye Ashley, alizaliwa mwezi Juni mwaka 2007. Fishburne ni mshabiki mkubwa wa Paulo Coelho na wamepanga kuigiza filamu inayotokana na kitabu cha hadithi cha The Alchemist.",
"Eric Wainaina\nWainaina alizaliwa mjini Nairobi, Kenya, na George Gitau Wainaina na Margaret Wangari Wainaina. Yeye ana ndugu mmoja, Simon Wainaina. Upendo wake wa muziki ulianza akiwa na umri mdogo. Alipata piano akiwa na umri wa miaka 4, iliyokuwa imenunuliwa kwa ajili ya ndugu yake Simoni ambaye alipendelea soka. Wainaina basi alichukua masomo katika piano shingo upande. Yeye walishiriki katika kwaya akiwa katika shule ya msingi na ya upili ya St Mary's, Nairobi, lakini kwa muda mfupi alicheza mchezo wa vikapu. Alipokuwa akikua, Wainaina aliathiriwa kimuziki na wasanii wa kimataifa, kama vile Papa Wemba, Youssou N'Dour, Lokua Kanza na Paul Simon."
] | 35
|
Je,sensa hufanyika nchini Kenya baada ya kila miaka ngapi?
|
[
"Sensa\nSensa ni utaratibu wa kupata na kutunza habari kuhusu idadi ya watu fulanifulani. Pia ni utaratibu wa mara kwa mara na hesabu rasmi ya idadi ya watu hao. Msamiati hutumiwa zaidi kuhusiana na idadi ya kitaifa na sensa ya mlango kwa mlango (kuchukuliwa kila miaka 10 kulingana na mapendekezo ya Umoja wa Mataifa), na ile ya kilimo na biashara."
] |
[
"Uchaguzi nchini Kenya\nUchaguzi Mkuu nchini Kenya hufanyika baada ya kila miaka mitano. Katika miaka ya hivi karibuni. Kenya imekuwa ikikumbwa na mizozo wakati wa uchaguzi, kwa mfano shuhudio la uchaguzi wa urais mnamo 2007. Ingawa mfumo wa vyama vingi ulianzishwa nchini mnamo 1992 na licha ya nchi hii kufanya uchaguzi tangu 1962, bado kuna matatizo makubwa ya taasisi za kisiasa ambayo huifanya hali kuwa vigumu kumaliza uchaguzi bila mizozo. .",
"Uchaguzi wa bunge nchini Kenya, 2007\nMnamo Mei 2009, Bunge lilihidhinisha kuundwa kwa Tume huru ya Uchaguzi ya mpito (IIEC), iliyosimamia uchaguzi mdogo katika majimbo ya Shinyalu na Bomachoge, ambao ulifanyika tarehe 27 Agosti 2009. Kiti cha Shinyalu kilibaki wazi wakati aliyekuwa mbunge wake Charles Lugano wa ODM aliaga dunia. ODM ilihifadhiwe kiti hicho, kufuatia ushindi wa Justus Kizito katika uchaguzi huo mdogo. Kiti cha Bomachoge pia kiliachwa wazi mara baada ya Uchaguzi wa 2007 katika jimbo kuvutiliwa mbali kufuatia udanganyifu. Kiti hiki kilikuwa kimeshindwa Joel Onyancha wa chama cha Ford-People katika uchaguzi mkuu wa 2007. Katika uchaguzi huu mdogo wa 2007 Simon Ogari wa ODM aliipuka mshindi huku akifuatwa kwa karibu na Joel Onyancha, ambaye wakati huu alikuwa akiwakilisha PNU Kwa mara ya kwanza nchini Kenya, vijisanduku vya uchaguzi vilivyotumikavilikuwa vimeundwa kwa kutumia vifaa vya uwazi (mtu angeweza kuona ndani ya vijisanduku)",
"Kenya\nKenya ina eneo kubwa wanapoishi wanyamapori likiwemo Masai Mara, ambapo nyumbu na wanyama wengi walanyasi hushiriki katika uhamaji kila mwaka. Uhamaji huo, hasa uhamaji wa nyumbu, hutokea Juni hadi Septemba na hushirikisha mamilioni ya wanyama. Tukio hili huwavutia sana wapigaji picha za sinema. Takribani nyumbu 250,000 huangamia kila mwaka katika uhamaji huu wa kutafuta lishe wakati wa kiangazi.",
"Uchaguzi Mkuu wa Kenya, 2007\nBaada ya Raila Odinga wa ODM kuongoza katika hesabu ya kura kwa muda mrefu Tume ya Uchaguzi ya Kenya lilisimamisha hesabu ya kura kwa muda wa usiku mmoja na baada kuanza upya kura za Mwai Kibaki wa PNU zilikuwa mbele. Tume ikamtangaza Kibaki kuwa mshindi aliyeapishwa mara moja bila kusubiri muda wa kisheria kwa malalamiko. Watazamaji waliona kasoro, makosa na matokeo yaliyodokeza ya kwamba hesabu ya kura ilibadilishwa kwenye ngazi za kupiga jumla za kura kimkoa na kitaifa. Vilevile kuna madokezo ya kwamba kura za kiraisi ziliongezwa katika usiku ambako hesabu ilisimamishwa.",
"Jangwa\nMto wa Ewaso Nyiro katika Kenya ya kaskazini kwa kawaida hukwisha katika nchi yabisi za Usamburu. Lakini kila baada ya miaka makumi kadhaa baada ya mvua kubwa sana inaendelea kuvuka jangwa la Somalia ya kusini na kufikia Bahari Hindi jinsi ilvyotokea wakati wa El-Nino 1998.",
"Cheti cha Masomo ya Msingi ya Kenya\nMtihani huu hufanyika wiki pili ya Novemba na inachukua siku nne tu. Kushahihishwa kwa mitihani inayohusisha kuandika (haya ni ya Insha ya Kiswahili na mtungo wa Kiingereza yaani Composition) hufanyika wakati ya likizo ya Desemba. Matokeo kisha hutangazwa na Waziri wa Elimu ya siku 3 au 4 baada ya siku ya Krismasi.",
"Seneti ya Kenya\nMwaka wa 2013, uchaguzi wa Seneti ulifanyika tarehe 4 Machi 2013. Chini ya katiba mpya, ambayo ilipitishwa wakati wa kura ya maoni ya mwaka 2010, uchaguzi mkuu wa 2013 ndio ulikuwa wa kwanza kujumuisha Maseneta wanaowakilisha kaunti 47. Ulikuwa pia uchaguzi mkuu wa kwanza wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).",
"KCSE\nMitihani wa KCSE hufanywa chini ya usimamizi wa hali ya juu ili kuepukana na vitendo vya udanganyifu na hudumu kwa muda wa\nmwezi mmoja. Kuna adhabu kali kwa visa vya udanganyifu kutoka Baraza la Mitihani ya Kitaifa ya Kenya na matokeo ya wanafunzi wanaoshikwa hutupiliwa mbali. Kwa kawaida, mtihani huanza 22 Oktoba na kumalizika mwishoni mwa Novemba. Kuanzia Desemba, mtihani husahihishwa na matokeo kutolewa 26 Februari mwaka unaofuata. Matokeo ya mitihani hutangaziwa umma na Waziri wa Elimu na wanafunzi na shule mia moja bora hufunuliwa vyombo vya habari siku iyo hiyo ya kutangaza. Upangaji wa shule bora hugawanywa katika shule binafsi, shule za umma na za mikoa. Kila kundi likiwa na shule mia moja bora.",
"Cheti cha Masomo ya Msingi ya Kenya\nKCPE ni ufupisho wa Kenya Certificate of Primary Education, tuzo la cheti kwa wanafunzi baada ya kuhitimu kwa kusoma miaka nane katika elimu ya msingi nchini Kenya. Mitihani yake husimamiwa na Kenya National Examination Council (KNEC), kitengo cha serikali cha kusimamia mitihani nchini Kenya, chini ya Wizara ya Elimu. Kitengo hicho pia husimamia na kufanyia mabadabiriko kwa Cheti cha Masomo ya Upili ya Kenya (KCSE), tuzo la cheti kwa wanafunzi baada ya kumaliza elimu ya sekondari. Vyeti vya KCSE na KCPE vilianzishwa nchini Kenya hapo mwaka wa 1985 wakatmfumo wa elimu wa 8.4.4 ulianzishwa. Maki za juu zaidi ni 500 lakini hiyo aghrabu haiwezekani kutokana na usawasaji (kutolewa kwa baadhi za alama katika kila somo).\nMtihani huu hutumiwa kuamua shule ya sekondari ambayo kila mwanafunzi atajiunga nayo.",
"Seneti ya Kenya\nKatiba ya Kenya ya 1963 ilitengeneza Seneti iliyokuwa na maseneta 41 waliochaguliwa kwa muda wa miaka sita, na theluthi moja ya wajumbe wa kustaafu kila baada ya miaka miwili. Timotheo Chokwe alikuwa spika wa kwanza wa Seneti hiyo. Seneti ilifanywa marufuku mwaka wa 1966, wakati wa uanachama wake uliunganishwa pamoja na ule wa Jumba la wawakilishi kuunda Bunge lenye chumba kimoja."
] | 11
|
Je,Mji mkuu wa Namibia ni upi?
|
[
"Windhoek\nWindhoek ni mji mkuu wa Namibia, na uko mahali pa 22.56 S 17.09 E. Idadi ya wakazi wake ni takriban 230,000. Mji huu ni kituo muhimu kwa biashara ya ngozi za kondoo. Zamani ulikuwa makao makuu ya mtemi wa kabila la Nama aliyewashinda kabila la Waherero wakati wa karne ya 19. Mwaka wa 1885, nchi ilivamiwa na wakoloni kutoka Ujerumani, na mji wa Windhoek ukawa makao makuu ya serikali ya ukoloni mwaka wa 1892. Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia nchi ilivamiwa na majeshi ya Makaburu kutoka Afrika ya Kusini ambao wametawala nchi ya Namibia hadi mwaka wa 1990. Namibia ilipopata uhuru, mji wa Windhoek ukawa mji mkuu wa Jamhuri ya Namibia.",
"Namibia\nMji mkuu ni Windhoek (wakazi 322.500)."
] |
[
"Mkoa wa Omaheke\nMkoa wa Omaheke ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 67,496 kwenye eneo la 84,732 km². Mji mkuu ni Gobabis.",
"Mkoa wa Ohangwena\nMkoa wa Ohangwena ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 227,728 kwenye eneo la 10,582 km². Mji mkuu ni Eenhana.",
"Mkoa wa Kunene\nMkoa wa Kunene ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 68,244 kwenye eneo la 144,255 km². Mji mkuu ni Opuwo.",
"Mkoa wa Caprivi\nMkoa wa Caprivi ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 79,852 kwenye eneo la 19,532 km². Mji mkuu ni Katima Mulilo.",
"Mkoa wa Omusati\nMkoa wa Omusati ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 228,364 kwenye eneo la 13,638 km². Mji mkuu ni Outapi.",
"Mkoa wa Erongo\nMkoa wa Erongo ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 107,629 kwenye eneo la 63,720 km². Mji mkuu ni Swakopmund.",
"Mkoa wa Oshikoto\nMkoa wa Oshikoto ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 160,788 kwenye eneo la 26,607 km². Mji mkuu ni Omuthiya.",
"Mkoa wa Otjozondjupa\nMkoa wa Otjozondjupa ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 135,723 kwenye eneo la 105,328 km². Mji mkuu ni Otjiwarongo.",
"Mkoa wa Oshana\nMkoa wa Oshana ni moja ya mikoa 13 ya kujitawala ya Namibia lenye wakazi 161,977 kwenye eneo la 5,290 km². Mji mkuu ni Oshakati."
] | 17
|
2pac Shakur aliuwawa akiwa na miaka ngapi?
|
[
"Tupac Shakur\nTupac Amaru Shakur (16 Juni 1971 - 13 Septemba 1996) alikuwa mwigizaji, mwanaharakati wa haki za binadamu, na pia mwanamuziki maarufu wa muziki wa hip hop kutoka nchini Marekani. Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama 2Pac. Ni mmoja kati ya wasanii wa hip hop waliouza rekodi nyingi za muziki dunia."
] |
[
"Me Against the World\nMwaka wa 1993, Tupac Shakur tayari alishakuwa na mafanikio katika tasnia ya muziki wa hip hop, akiwa na kwa ajili ya single zake zilizompeleka katika ishirini bora kwa chati za pop (\"I Get Around\", \"Keep Ya Head Up\"), na kwa albamu mbili ambazo zimeweza kushika ishirini-na-tano bora za \"Billboard\" 200 (\"Strictly 4 My N.I.G.G.A.Z.\"). Hata hivyo, msanii huyu mwenye umri wa miaka 22 amepata kuwa na mfululizo wa matukio na kushtakiwa kwa makosa kadha wa kadha ya uvunjaji wa sheria.",
"A 2Pac Tribute: Dare 2 Struggle\nDr. Mutulu Shakur (baba asiyemzazi wa Tupac) alitoa albamu hii kama kumbukumbu ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa Tupac na maadhimisho ya miaka kumi ya kufa kwake. Albamu umeshirikisha marapa mbalimbali walio jela na wengine wa nje, ikiwa ni pamoja na watoto wa Mutulu Shakur, Mopreme Shakur na Nzingha, vilevile Outlawz, TQ, Slick, Imaan Faith na T-Jay. Awali ilitungwa kabla kuuawa Tupac 1996, wakati yeye na Mopreme walipoenda kumtembelea baba yao jela na kuandika \"Thug Code\" kwa lengo la kujaribu kupunguza vitendo vya kihuni.",
"Me Against the World\nMnamo mwezi wa Novemba, Shakur na wenzake wawili wa katika msafara wake walishtakiwa kwa kosa la ubakaji wa mshabiki wao wa kike, tukio ambalo walikutwa na makosa na hatimaye kutumikia kifungo cha miaka 4.5 jela. Kulingana na maelezo ya Shakur, albamu ilitengenezwa kwa ajili ya kuonesha wapenzi wa hip hop heshima zake katika sanaa hiyo. Kimashairi, Shakur kimakusudi alijaribu kutengeneza hii kibinafsi zaidi, makini, na juhudi kupita albamu zile za awali.",
"Beginnings: The Lost Tapes 1988–1991\nAlbamu ilitayarishwa na mmoja wa wanakundi la Digital Underground, Chopmaster J, \"Beginnings...\" ni mkusanyiko wa nyimbo zake za mwanzoni kabisa, ilitengenezwa kabla Shakur hajaanza kuifanyia kazi albamu yake ya kwanza, \"2Pacalypse Now\". \nCD Universe walieleza ya kwamba \"uimbaji wa Shakur na maudhui ya mashairi yake ni kumbukumbu ya waimbaji waliotamba mwisho/mwanzoni mwa miaka ya 1980s/1990 kama kina Big Daddy Kane na Rakim\" kuliko hata nyimbo zake mwenyewe 2Pac za baadaye. Jason Birchmeier wa Allmusic alikubali ya kwamba rapa huyu anaonekana \"kuvutia zaidi hapa, shaka hakuna, lakini hata hivyo mzito kidogo na anagezea\". Birchmeier nae pia alieleza yake ya kwamba \"kuna jambo hapa kidogo kuliko lile fuvu la mashine ya utayarishaji wa biti\".",
"Tupac Shakur\nHuyu alikuwa mtoto wa Afeni Shakur, ambaye alikuwa mwanachama wa chama cha Black Panther Party. Mama yake Tupac alitolewa jela mwezi mmoja kabla ya kumzaa Tupac. Tupac alikufa mnamo tar. 13 Septemba katika mwaka wa 1996 baada ya kupigwa risasi akiwa anaendesha gari mjini Las Vegas, Nevada, siku saba kabla kifo chake.",
"Me Against the World\nWakati wa kiangazi cha mwaka wa 1993, Shakur alishtakiwa kwa kosa la kumshambulia mwongozaji Allen Hughes wakati wanapiga filamu ya \"Menace II Society\"; Shakur baadaye akahukumiwa kifungo cha siku 15 jela. Baadaye, mnamo mwezi wa Oktoba 1993, Shakur alishtakiwa kwa kosa la kuwatandika maofisa wawili wa polisi ambao walikuwa hawapo-kazini huko mjini Atlanta, kulingana na jinsi mashtaka yaliyo hatimaye kesi ikafutwa.",
"Big Pun\nJuhudi zake katika muziki zilikujakwisha katika mwaka wa 2000 akiwa na umri wa miaka 28. Big Pun alikufa kwa shinikizo la . Bwana huyu ameacha mke, Liza Rios, na watoto watatu. Anakadiriwa kuwa alifariki akiwa na uzito wa paundi 700 ambazo ni sawa na kilogramu 300. Kila kitu kuanzia kuoga na kuvaa hadi viatu, alikuwa akisaidiwa kufanya shauri ya uzito mkubwa aliokuwa nao.",
"Diskografia ya Tupac Shakur\nHii ni diskografia ya Tupac Shakur, rapa kutoka nchini Marekani. Kumepata kutolewa albamu takriban kumi na moja; nne zilitolewa kabla ya kifo cha Shakur mnamo Septemba 13, 1996 na saba zilitolewa baada ya kifo chake, ya kwanza ikiwa \"The Don Killuminati: The 7 Day Theory\" ilitolewa mnamo Novemba 5, 1996 (ijapokuwa albamu ilikamilika kabla hata Shakur hajafa). Tupac Shakur ameuza nakala za rekodi milioni 75 kwa hesabu ya dunia nzima,",
"I Wonder If Heaven Got a Ghetto\nKwenye muziki wa video, taswara ya kwanza ya kamera ineonesha mtu akielezea mawazo na mitazamo ya Shakur. Baada ya kupigwa risasi, ameanguakia kwenye jumba la Masista lililoitwa Rukahs ('Rukahs' ni 'Shakur' imeandikwa kinyumenyume), huko mjini New Mexico. Leseni ya bamba la gari ambalo Shakur ameingia na mzee linasoma \"61671\", ambapo inataja tarehe ya kuzaliwa kwa Shakur mnamo 16 Juni 1971. Chumba alichoingia na msichana ni namba 7. Saa iliyokuwa kwa nyuma inaishia 4:03, ni muda rasmi aliokufa Shakur. Mwishoni kabisa, ameenda kwa Amaru Diner, Amaru likiwa jina lake la kati."
] | 40
|
Edith Chewangel Masai alizaliwa wapi?
|
[
"Edith Masai\nMasai alizaliwa katika kijiji cha Chepkoya, wilaya ya Mlima Elgon. Alishindana wakati wake wa shule ya sekondari wakati alikuwa katika shule ya upili ya Kibuk. Alihitimlu kutoka skuli hiyo mwaka wa 1988. Alijiunga na Kenya Prisons Service mwaka wa 1990, inayojulikana sana kwa kusajili wanariadha wengi wenye vipaji. Masai hata hivyo, hakupata chochote hadi mwaka wa 1999, wakati akawa bingwa wa mbio za kuvuka nchi au “cross-county” ukipenda,akiwa na umri wa miaka 32. Baada ya ushindi huu, alianza kufanya mazoezi zaidi kwa umakini"
] |
[
"Edith Masai\nEdith Chewangel Masai (alizaliwa mnamo 4 Aprili 1967) ni mwanariadha kutoka Kenya. Mafanikio yake bora ni medali tatu za dhahabu za kibinafsi katika mashindano ya dunia ya kuvuka nchi ya IAAF kati ya mwaka wa 2002 na 2004. Pia anajulikana kwa kufikia mpaka wa kimataifa akiwa na umri wa miaka 35.",
"Edith Masai\nEdith alishinda medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya mwaka wa 2003. Mwaka wa 2004 alishindwa katika majaribio ya Kenya kushiriki katika michezo ya Olimpiki, lakini tangu alikuwa mmoja wa Wakenya watatu tu ambao walikuwa wameishinda wakati wa kufuzu wa Olimpiki \"A\"- katika mbio ya mita 5000 ya wanawake mwaka huo, alipewa nafasi kwenye timu. Masai mwenyewe awali alikuwa ameikataa fursa hiyo, lakini alijiunga na timu baada ya mazungumzo marefu. Katika Michezo ya Olimpiki alijiondoa mashindanoni kwa kulalamikia jeraha la “hamstring”.",
"Edith Masai\nEdith alishinda medali ya fedha katika mbio ya mita 10000 katika Michezo ya All-Africa mwaka wa 2007. . Muda wake wa dakika 31:31.18 ni rekodi mpya ya Dunia kwa mwanamke aliye na umri zaidi ya miaka 40. Rekodi ya hapo awali ilikuwa inashikiliwa na Nicole Leveque wa Ufaransa, ambaye alikimbia kwa muda wa dakika 32:12.07 katika mji mkuu wa Helsinki mwaka wa 1994. Masai alishiriki katika marathon ya mashindano ya dunia mwaka wa 2008 katika mji mkuu wa Osaka nchini Japani, na kumaliza katika nafasi ya 8 katika mbio ambayo ilishindwa na mkimbiaji mwenzake Catherine Ndereba.",
"Édith Piaf\nEdith Piaf (19 Desemba 1915 – 11 Oktoba 1963) alikuwa mwimbaji nchini Ufaransa aliyependwa sana na wananchi.\nJina lake la kuzaliwa ni Edith Giovanna Gassion lakini alichukua jina la kisanii \"Piaf\" (kifaransa kwa ndege shomoro). Wazazi walikuwa wahamiaji kutoka Italia, bibi yake upande wa mama alikuwa berberi kutoka Afrika Kaskazini. Wazazi hawakumtunza walimwachia kwa bibi upande wa baba na huyu alioongoza nyumba ya makahaba mjini Bernay (Normandie). Hapa alitunzwa na makahaba; kuna kumbkumbu ya kwamba alionjeka alipokuwa na miaka 5 akawa kipofu lakini makahaba wote walisimamisha kazi yao kwa siku tatu wakamwombea kanisani akaponyeka.",
"Chiwale\nMwaka huohuo wa 1965, jitihada za kuhamia zilianza ndipo walipata gari la tajiri mmoja aliyekuwa akijulikana kwa jina la Govind toka mjini Masasi, na hivyo kuweza kuhamisha mizigo yao hadi sehemu iitwayo Nangose (Marokopaleni), kwa mwalimu Karlo, kwa sababu hapakuwepo na njia/barabara ya kupita gari. Kazi ya kuhamisha mizigo kwa kichwa ilikamilika ndani ya mwaka huohuo wa '65, na familia ikawa imehamia rasmi Chiwale.\nWaliokuwepo katika msafara huo ni hawa wafuatao;\n1. Mwinyi mzee Makolela\n2. Bi. Aluna Maulana (mke wa mwinyi Makolela)\n3. Bi. Hadija Izulu\n4. Bw. Suedi Sandali\n5. Bw. Thabiti Makolela\n6. Bw. Bashiri Makolela\n7. Bi. Hadija Makolela\n8. Bi. Rukia Makolela\n9. Bi. Dunia Makolela\n10. Bw. Waziri Makolela\n11. Bw. Abdalla Makolela",
"Chiwale\nKijiji cha Chiwale kilipata usajili wa kudumu kama kijiji rasmi cha ujamaa kati ya miaka ya 1973-1975, hivi, wakati huo kilikuwa na wakazi takribani 200 wengi wao wakiwa ni wahamiaji kutoka katika vijiji vya kusini mwa Masasi na wengine Msumbiji. Viongozi wa kwanza wa kijiji wakiwa ni Edmundi Akili, (Katibu wa kijiji), Muhidin Alias (Mwenyekiti), Mfaume Hassan Hinchuppi (Mkuu wa mabalozi wa nyumba kumi), pamoja na viongozi wengine. Mwaka 1973, ilianzishwa shule ya msingi ambapo mwalimu Edward George Kazibure alihamishiwa kutoka Lukuledi kwa madhumuni ya kuanzisha shule hiyo.",
"Edith Masai\nTangu wakati huo Masai ameacha kukimbia mbio za “track” na ameanza kukimbia mbio za marathon. Masai alishinda Marathon ya Hamburg mwaka wa 2005 na alishiriki katika marathon hiyo katika miaka ya 2006 na 2007. Mwaka wa 2006 aliibuka mshindi katika marathon nusu ya Berlin, kuweka muda wa kasi zaidi katika nusu marathon iliyokimbiwa mwaka huo, dakika 1:07:16. Pia ilikuwa muda bora wa kibinafsi na rekodi ya kozi. Pia aliweka rekodi mpya ya Kenya ya mita 5000 kwa muda wa dakika 14:33.84.",
"Edith Masai\nEdith alimaliza katika nafasi ya 5 katika mbio za mita 10000 katika mashindano ya dunia yaliyofanyika katika mji mkuu wa Helsinki mwaka wa 2005 nchini Finland. Muda wake wa dakika 30:30.26 ulikuwa rekodi mpya ya Kenya Rekodi hiyo ilivunjwa na Linet Masai katika Michezo ya Olimpiki mwaka wa 2008, ambaye alikimbia kwa muda wa dakika 30:26.50",
"Zauditu wa Ethiopia\nZauditu (29 Aprili 1876 – 2 Aprili 1930) alikuwa malkia mtawala wa Uhabeshi kuanzia 27 Septemba 1916 hadi kifo chake. Alimfuata Iyasu V. Jina lake la kubatizwa lilikuwa \"Askala Maryam\". Alikuwa mtoto wa kwanza wa Menelik II. Mwanzoni utawala wake ulisumbuliwa na uasi wa Iyasu aliyekuwa ameuzuliwa. Malkia huyu anajulikana kwa jinsi alivyopenda dini na alivyokuwa mpinzani mkubwa wa mabadiliko aliyokuwa akiyafanya Ras Tafari Makonnen. Zauditu aligombana sana naye Makonnen, kuhusu mambo ya siasa lakini alishindwa. Naye Tafari alimfuata kama mfalme chini ya jina la Haile Selassie."
] | 35
|
Nani rais wa shirikisho la FIFA duniani?
|
[
"FIFA\nKisheria ni shirika binafsi lililoandikishwa huko Uswisi. Makao makuu yapo Zurich. Rais Joseph Blatter ameongoza kwa muda wa miaka 18 kabla ya kumuachia Gianni Infantino, raia wa Uswisi. Fatma Samba Diouf Samoura wa Senegal ndiye Katibu Mkuu wake."
] |
[
"FIFA kombe la shirikisho la Mabara 2009\nFIFA kombe la shirikisho la Mabara 2009 lilikuwa kombe ka shirikisho, la mara ya nane na lilifanyika Afrika ya Kusini kuanzia 14 Juni - 28 Juni 2009 likifatia Kombe la Dunia la FIFA 2010. Droo ilifanyika tarehe 22 Novemba 2008 kwenye ukumbi wa Sandton Convention Centre mjini Johannesburg. Mechi ya ufunguzi ilichezwa katika uwanja wa Coca-cola park mjini Johannesburg. Brazili, ilishinda michuano hii ambapo walitetea kikombe ambacho walikinyakua tena mwaka 2005 kwa kuwafunga Marekani magoli 3-2 katika fainali.",
"Nani\nNani alifunga katika dakika ya 10 katika FA Community Shield mwaka wa 2009, lakini United ilipoteza mechi hiyo kupitia mikwaju ya penalti kufuatia sare ya 2-2. Nani alijeruhiwa begani wakati wa mechi hiyo, ambayo awali ilitarajiwa kumweka hadi mwanzo wa msimu, lakini alipona na kuichezea Ureno dakika 17 dhidi ya Liechtenstein tarehe 12 Agosti, na kuanza mechi dhidi ya Birmingham City tarehe 16 Agosti. Ingawa aliandaa pasi lililomsababisha Wayne Rooney kufunga bao la ushindi katika dakika ya 34, Ryan Giggs aliingia kama mbadala wake baada ya nusu ya kwanza ya mechi. ] Kuondoka kwa Cristiano Ronaldo kwenda Real Madrid kulimaanisha kuwa kungekuwa na wachezaji wengi ambao wangetaka kuchukua majukumu ya “free-kick” na Nani alichapa na kufunga bao lake la kwanza la msimu wa 2009-10 kutoka kwa “free-kick” dhidi ya Wigan athletic, katika ushindi wa 5-0 ugenini.",
"Nani\nMechi ya kwanza ya Nani ya ligi kuu ya Uingereza ilikuwa katika mechi ya ufunguzi ya nyumbani, Manchester United ikiwa mwenyeji wa Reading tarehe 12 Agosti na Nani aliingia kama mbadala kwa Wayne Rooney, ambaye alipata jeraha la mguu. Manmo 26 Agosti 2007, Nani alifunga bao lake la kwanza la ushindani la Manchester United, bao la ushindi kutoka yadi 30 katika dakika ya 69 dhidi ya Tottenham Hotspur. Pia Nani aliandaa mabao muhimu kwa Louis Saha na Nemanja Vidic na kuruhusu Manchester United kuzicharaza Everton na Sunderland 1-0. Pia alifunga bao maarufu dhidi ya Middlesbrough, ambayo ilianzisha ushindi wa 4-1. Hii ilikuwa mechi ya kwanza ambayo ilidhaniwa kwamba Wayne Rooney na Carlos Tevez walionyesha ahadi ya kwanza ya kweli ya kufomu ushirikiano mzuri. Alirudi kwa klabu yake ya zamani, Sporting, katika mechi ya ligi ya Mabingwa barani Ulaya mwezi wa Septemba, ingawa ilikuwa mwenzake na mchezaji wa zamani wa Sporting Cristiano Ronaldo ambaye alifunga bao la ushindi katika ushindi wa 1-0.\nMnamo 16 Februari 2008, Nani alikuwa mchezaji bora katika mechi dhidi ya Arsenal katika raundi ya nne Kombe la FA, bao lake na pasi mbili alizoziandaa zilizosababisha mabao ziliisaidia United kushinda mechi hiyo 4-0 dhidi ya wapinzani wao jadi. Katika mechi hiyo, Nani alihusika katika ubishi pamoja na nahodha William Gallas wa Arsenal ambaye aliona kwamba Mreno alikuwa \"anamadharau\". Baada ya mechi, pia Arsène Wenger hakuwa amefurahishwa na kitendo cha Nani huku Gilberto Silva akisema kuwa Nani alikuwa na \"kuchwa kubwa (ujeuri)\".",
"Nani\nNani alikuwa mwanachama wa kawaida wa kikosi cha Kireno katika mechi za kufuzu kushiriki katika Euro 2008 UEFA, na alifunga bao moja kati ya mbili katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Ubelgiji tarehe 2 Juni 2007. Pia alimwandalia pasi safi mchezaji mwenzake Ricardo Quaresma aliyefunga bao katika mechi ya kirafiki dhidi ya Italia tarehe 6 Februari 2008. Fomu ya Nani kwa Manchester United wakati wa msimu wa 2007-08 hatimaye ilimwezesha kupata mwito kwa kikosi cha wachezaji 23 cha Luiz Felipe Scolari kwa ajili ya Euro 2008, pamoja na mchezaji mwenzake wa klabu Cristiano Ronaldo. Nadra alitumika katika kampeni hiyo, lakini aliweza kuanda pasi safi iliyomsababisha Helder Postiga kufunga bao baada ya kuingai katika dakika 15 za mwisho katika robo fainali dhidi ya Ujerumani tarehe 19 Juni 2008. Ureno hatimaye ilipoteza mechi hiyo 3-2.",
"Kombe la Dunia la FIFA 2018\nKombe la Dunia la FIFA 2018 ilikuwa michuano ya 21 ya Kombe la Dunia la FIFA inayohusisha timu za taifa za wanaume katika mchezo wa soka. Michuano hii ilishirikisha timu za wanaume kutoka nchi mbalimbali duniani ambazo ni wanachama wa FIFA na hufanyika mara moja kila baada ya miaka minne. Ilifanyika nchini Urusi ikaanza tangu tarehe 14 Juni na kilele cha michuno hii kilikuwa 15 Julai 2018 ambapo timu zilizoingia fainali Ufaransa na Kroatia zilicheza kuamua bingwa wa dunia. Ufaransa ilishinda kwa 4:2.",
"Mpira wa miguu\nShirikisho la Soka Duniana (FIFA) ndilo shirikisho kuu linalosimamia kandanda duniani. Wanachama wake ni mashirikisho ya kandanda ya nchi mbalimbali. Kufikia mwaka wa 2000, lilikuwa na wanachama 204 kutoka pembe zote za dunia. Shirikisho hili huandaa mashindano mbalimbali ya soka kama vile Kombe la Dunia la FIFA na pia huwatunuku wachezaji.",
"FIFA kombe la shirikisho la Mabara 2009\nDroo ya mashindano ilifanyika tarehe 22 Novemba 2008 \"Sandton Convention Centre\" mjini Johannesburg. Kila timu ilikuwa inawakilishwa katika droo na mshindani wake katika Miss World 2008 isipokuwa kwa Iraq, ambayo iliwakilishwa na mrembo wa dunia 2007, Zhang Zilin, kutoka Jamhuri ya Watu wa China. Timu ziligawanywa katika makundi miwili:",
"FIFA\nTarehe 27 Mei 2015 polisi ya Uswisi ilikamata maafisa 7 wa FIFA, kati yao makamu 2 wa rais Blatter, katika hoteli ya mjini Zurich walipokusanyika kwa mkutano wa Kamati Kuu. Polisi ilitekeleza hati ya kifungo ya tarehe 21 Mei 2015 kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Marekani aliyeamua kuwashtaki kwa udanganyifu, ulanguzi na kuficha fedha zisizo halali. Mashtaki yalifunguliwa rasmi dhidi ya maafisa 9 wa FIFA, mameneja 4 wa makampuni ya kuuzia huduma na vifaa vya michezo na mfanya biashara mmoja.",
"Sepp Blatter\nSepp Blatter ni msimamizi wa soka wa Uswisi ambaye alikuwa rais wa nane wa Chama cha FIFA mwaka 1998 hadi mwaka 2015. Blatter akawa katibu mkuu wa FIFA mwaka wa 1981 na kisha alichaguliwa rais katika Shirikisho la 51 la FIFA mnamo 8 Juni 1998, akiwa na João Havelange, ambaye alikuwa amesimama shirikani tangu 1974.",
"UEFA\nUEFA ndilo shirikisho la bara kubwa zaidi katika FIFA kwa sita yaliyomo. Kati ya mashirikisho yote, kwa mbali ndilo lenye nguvu zaidi katika masuala ya mali na ushawishi katika ngazi ya klabu. Karibu wachezaji wote mashuhuri wa soka ulimwenguni hucheza katika ligi za Uropa, kidogo kwa sababu ya mishahara inayopatikana kutoka vilabu tajiri zaidi duniani, hasa katika Uingereza, Uhispania, Italia na Ujerumani. Nyingi ya timu za kitaifa zenye nguvu zaidi duniani ziko katika UEFA. Katika nafasi 32 zilizoko katika Kombe la Dunia la FIFA 2010, 13 zilitengewa timu za mataifa ya UEFA, na kwa sasa 12 ya timu bora 20 kulingana Orodha ya FIFA ya Dunia ni wanachama wa UEFA."
] | 56
|
Je,Bill Gates ana watoto wangapi?
|
[
"Bill Gates\nBill Gates alifanya ndoa na Melinda French Gates mwaka wa 1994 na wakabarikiwa na watoto watatu, Jennifer, Rory na Fibi. Wote wawili Bill na Melinda ni waanzilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali. Waliweza kulianzisha shirika la Bill na Melinda Gates Foundation ambalo limeweza kuchangia zaidi ya dola bilioni tatu nukta mbili kuboresha afya duniani, dola bilioni mbili kuboresha fursa ya masomo kwa familia zisizojiweza. Zaidi ya hayo limeweza pia kuchangia dola milioni mia nne sabini na saba kwa miradi ya jamii na zaidi ya dola milioni mia nne themanini na nane kwa miradi maalum na kampeni za kuhamasisihwa kila mwaka."
] |
[
"Bill Gates\nBill Gates pia ana maslahi katika biashara nyingine akiwa na nafasi nyingi za uwekezaji na vyeo katika kampuni tofauti ikiwemo Corbis Corporation, Berkshire Hathaway Inc, Teledesic Corporation. Mwaka wa 1998 Gates alijitoa jukumu lake kama Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Microsoft na kuzingatia maendeleo ya teknolojia na bidhaa mpya.",
"Bill Gates\nWilliam Gates III H anajulikana kama Bill Gates alizaliwa tarehe 28 Oktoba 1955 na kulelewa katika kijiji cha Seattle pamoja na dada zake wawili. Katika umri wake mdogo Bill Gates alivutiwa na utengenezaji wa programu akiwa katika mojawapo wa shule kijijini Seattle. Akiwa huko shuleni Seattle, Bill Gates alikutana na Paul Allen, mwanafunzi mwenzake wakawa marafiki. Hapo ndipo wakaanza kutumia tarakilishi ndogo ya shule kujiendeleza ujuzi wao.",
"Bill Gates\nBill Gates ni mwanzilishi, mwenyekiti na mbunifu mkuu wa programu za kampuni ya ya Microsoft, kampuni ya programu yenye mafanikio zaidi duniani, inayoaminika kwa utengenezaji wa programu zilizo na nguvu na ubunifu hali zikiwa bado zenye utumizi mwepesi. Microsoft sasa inaajiri zaidi ya watu elfu hamsini na tano katika nchi themanini na tano.",
"Bill Gates\nWalijiunga na kampuni ya kompyuta, malipo yao ikiwa ni kutumia tarakilishi yenye nguvu zaidi. Kazi yao ilikuwa ni kutafuta nukshi katika mitambo ya kompyuta, wakati huohuo waliweza kijifunza lugha mpya za kompyuta. Bill akaenda kwenye Chuo Kikuu cha Harvard. Kwa mara nyingine tena akajiunga pamoja na Paul kuandika toleo jipya la programu ya Msingi wa lugha ya kwanza ya kompyuta ya kibinafsi, iitwayo Altair 8800. Kampuni hiyo iliridhishwa na kazi ambayo Bill Gates na Paul Allen waliofanya na programu hiyo ikapewa leseni. Jambo hili liliwachangia Gates na Allen kuanzisha kampuni ya Microsoft, iliyokuwa ikitengenezea kampuni zingine programu. Bill Gates aliacha masomo yake katika chuo kikuu cha Harvard na kujishughulisha muda wake wote katika biashara.",
"Bill Gates\nKatika mwaka wa 1990 Microsoft ikiongozwa na Bill Gates ilitoa toleo jipya la Windows liitwayo Windows 3.0 na kuboreshwa kiasi GUI. Toleo hili jipya liliweza kuuzwa zaidi ya nakala milioni kumi, likifuatiwa na matoleo mengine ya Windows 3.1, 3.11 na makundi ya kazi ambayo yaliongeza misaada kwa mitandao. Kutokana na mafanikio yao ya maendeleo, Microsoft ilitoa matoleo mengine ya Windows 95 ikifuatiwa na Windows 98, 2000, Millennium Edition na toleo la sasa Windows XP. Kila toleo jipya lilipotolea kampuni ya Microsoft ilizidi kupata umaarufu katika soko la hisa, ikiongezwa na baadhi ya programu kama vile Microsoft Office, michezo n.k. Umaarufu huu umemfanya Bill Gates kuwa mtu tajiri duniani myenye thamani ya wastani wa dola bilioni arubaini na sita.",
"Bill Gates\nKipindi cha miaka mitano baadaye Microsoft ilitoa mifumo mipya ya Windows 2.0 iliyokuwa bora zaidi kuliko mifumo ya hapo awali. Kampuni ya Microsoft iliweza kupata umaarufu zaidi katika soko la hisa, na akiwa umri wa miaka 31, Bill Gates aliweza kuwa bilionea mchanga zaidi katika historia ya Marekani.",
"Bill Gates\nMicrosoft ilitangaza mfumo mpya wa uendeshaji wa kompyuta uitwao Windows 1.0 mwaka wa 1983, ambao ulikuwa na grafiksi bora na pia uliwezesha kufanya zaidi ya jambo moja kwa wakati mmoja. Hata hivyo hakuwa bidhaa nyingine iliyotolewa miaka mbili baadaye hadi mwaka wa 1985, kwa kuwa ni programu chache zilizoweza kuendeshwa katika mfumo huu wa Windows 1.0. Hivyo mfumo huu mpya haukupata umaarufu vile.",
"Bill Gates\nBill Gates - (William Henry Gates III) Mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft, mtu tajiri sana duniani na mwanzilishi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Bill and Melinda Gates Foundation.",
"Bill Gates\nMapumziko yao yalikuja walipotengeneza mfumo wa kuendesha kompyuta uitwao MS-DOS uliotumika katika kompyuta ya kwanza ya kibinafsi ya IBM. Baadaye waliweza kuzishawishi kampuni zingine zinazotengeneza kompyuta kutumia mfumo huo wa MS-DOS. Mfumo huu mpya wa MS-DOS ulipata umaarufu katika soko miaka ya 1980 na baadaye, Microsoft pia ilianza kutengeneza programu kama vile neno sindikizi."
] | 8
|
Otto Von Bismarck alizaliwa wapi?
|
[
"Otto von Bismarck\nJina lake kamili lilikuwa Otto Eduard Leopold von Bismarck-Schönhausen. Alizaliwa katika familia ya kitemi wa cheo cha chini katika ufalme wa Prussia, mama yake alikuwa wa asili ya kiraia."
] |
[
"Otto von Bismarck\nBismarck alikuwa kiongozi wa Ujerumani wakati nchi za Ulaya ziliendelea kujipatia pande kubwa za dunia kama koloni. Mwanzoni alipinga makoloni kwa Ujerumani. Aliona gharama kubwa za kupata, kujenga na kutetea koloni akaona ya kwamba faida yoyote ya kuwa nazo hailingani na gharama hizo.",
"Otto von Bismarck\nBismarck alilenga sasa kukamilisha kipaumbele cha Prussia katika Ujerumani. Alitumia nafasi ya magongano na Ufaransa juu ya uchaguzi wa mfalme mpya wa Hispania. Kaisari Napoleon III wa Ufaransa alitaka Mfaransa achaguliwe lakini Bismarck alimsukuma mgombea Mjerumani. Katika vita ya maneno ya kidiplomasia chansella aliweza kumwaibisha mtawala wa Ufaransa. Napoleoni III alitangaza hali ya vita dhidi ya Prussia lakini madola ya Ujerumani ya Kusini, kama falme za Bavaria na Wuerttemberg, yalijiunga na Prussia.\nVita hii ilikuwa mara ya kwanza ya kwamba Wajerumani wote -isipokuwa Austria- walishikamana pamoja tangu muda mrefu sana. Bismarck alitumia nafasi ya ushindi wa jeshi la Wajerumani kuwakusanya viongozi wa madola yote ya Ujerumani katika jumba la Kifalme la Ufaransa huko Versailles. Mfalme wa Prussia Friedrich Wilhelm IV alitangazwa kuwa Kaisari Wilhelm I wa Ujerumani - cheo hiki hakikutumika katika Ujerumani tangu mwaka 1806. Dola la Ujerumani liliunganisha madola yote ya Ujerumani ya kale, isipokuwa Austria, chini ya mfalme wa Prussia aliyekuwa sasa pia na cheo cha Kaisari wa Ujerumani.",
"Otto von Bismarck\nMwaka 1851 mfalme wa Prussia alimteua kuwa mwakilishi wa Prussia katika halmashauri ya Shirikisho la Kijerumani huko Frankfurt - wakati ule Ujerumani ilikuwa shirikisho lisilo na nguvu ya madola 38 yaliyojitegemea. Madola makubwa katika shirikisho hili yalikuwa Austria na Prussia. Bismarck alikuwa pia na vipindi vifupi vya utumishi kama balozi wa Prussia huko St. Petersburg na Paris.",
"Otto von Bismarck\nTangu mwaka 1880 Bismarck alitegemea bungeni vyama vya kisiasa vilivyotaka kuunda makoloni, hivyo alilegea na polepole kukubali kuanzishwa kwa makoloni kadhaa. Mwanzoni alitoa tu nyaraka za ulinzi kwa makampuni yaliyopatana kukodi maeneo na watawala wa Afrika na wa Pasifiki.",
"Otto von Bismarck\nTangu miaka ya 1870 iliongezeka idadi ya watu katika Ujerumani waliodai koloni kwa sababu mbalimbali. Wengine walidai koloni kama ishara ya nchi kubwa na muhimu, wengine walikuwa wafanyabiashara waliotafuta ulinzi wa manowari za Kijerumani kwa ajili ya biashara yao dhidi ya wenzao wa mataifa mengine. Bismarck aliona ya kwamba hali ya Ujerumani haitegemei kuwepo kwa bendera yake katika pembe za dunia, bali uhusiano na majirani makubwa katika Ulaya hasa Uingereza, Ufaransa na Urusi. Tamko maarufu alipotembelewa na mgeni aliyetaka kumhamasisha kuunda koloni katika Afrika likawa \"Ramani yako ya Afrika ni ya kuvutia sana. Lakini ramani yangu ya Afrika iko Ulaya. Ufaransa iko upande wa kushoto, Urusi upande wa kulia, katikati tuko sisi\".",
"Otto von Bismarck\nMwaka 1862 aliteuliwa na mfalme Friedrich Wilhelm IV kuwa waziri mkuu wa Prussia. Shabaha yake kuu ilikuwa kuongeza uwezo wa nchi. Aliimarisha jeshi la Prussia dhidi ya upinzani wa wabunge wengi. Jeshi hilo lilipewa nafasi ya kuonyesha uwezo wake katika vita dhidi ya Denmark ya mwaka 1864. Matokeo ya vita yaliongeza mashindano kati ya Prussia na Austria juu ya kipaumbele ndani ya Shirikisho la Kijerumani.",
"Prussia\nKatika ya vita ya wenyewe kwa wenyewe katika Ujerumani 1866 Prussia ilishinda Austria na kuwa dola kiongozi kati ya madola ya Ujerumani. Mwanasiasa mkuu wa nyakati zile alikuwa Otto von Bismarck kama waziri mkuu wa Prussia na baadaye kama chansella wa Ujerumani.\nBaada ya kushinda Ufaransa katika vita ya 1871 sehemu zote za Ujerumani isipokuwa Austria ziliunganika chini ya uongozi wa Prussia na kuanzisha Dola la Ujerumani. Mfalme Wilhelm I wa Prussia alichaguliwa kuwa Kaisari wa Ujerumani. Alifuatwa na mtoto wake Friedrich III aliyekufa mapema halafu na Wilhelm II. Wakuu wale walitawala kwa cheo cha \"Kaisari ya Ujerumani na mfalme wa Prussia\".",
"Otto von Bismarck\nOtto von Bismarck (1 Aprili 1815 – 30 Julai 1898) alikuwa mwanasiasa mashuhuri wa Ujerumani katika karne ya 19.",
"Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki\nMwanzoni Peters alikataliwa na serikali ya chansella Bismarck ambaye hakuona faida ya kuunda koloni akaogopa hasara. Lakini Peters aliitisha serikali ya kwamba angeweza kuuza maeneo yale kwa mfalme Leopold II wa Ubelgiji aliyejenga wakati uleule koloni yake katika Kongo. Hapa Bismarck aliogopa wanasiasa katika bunge waliowahi kudai koloni za Ujerumani eti wangesema kwa nini mtu mwema anayetaka kutupatia koloni amedharauliwa na sasa wageni wa Ubelgiji wamepata faida. Hivyo Peters alipewa hati ya ulinzi kutoka serikali ya Berlin iliyosema ya kwamba maeneo yote yaliyotajwa katika mikataba yako chini ya ulinzi wa serikali ya Ujerumani.\nBaada ya kupokea hati ya serikali Peters na wenzake waliunda Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki na kuhamisha haki za Shirika chini ya sheria ya Ujerumani kwa Kampuni.",
"Kaisari Wilhelm I\nKutokana na ugonjwa wa mfalme alianza kutawala Prussia tangu 1857 na baada ya kifo cha kaka alipokea taji la mfalme tarehe 2 Januari 1861. Mwanzoni alipendelea siasa ya upatanisho na bunge la Prussia lakini lilipokataa kumpa pesa kwa ajili ya jeshi jinsi alivyotaka aliachisha serikale yake na kumpa Otto von Bismarck madaraka ya waziri mkuu. Pamoja na Bismarck alifuata mipango yake ya kijeshi hata bila kibali cha bunge.",
"Afrika ya Mashariki ya Kijerumani\nHadi mnamo mwaka 1880 serikali ya Ujerumani chini ya chansella Otto von Bismarck ilikataa kuanzisha makoloni. Sehemu ya wafanyabiashara Wajerumani walidai koloni. Walisikitika kuona faida za wenzao Waingereza waliopata mara nyingi msaada kutoka kwa wanajeshi na serikali za koloni za Uingereza hasa Asia. Waliona pia faida ya viwanda vya Uingereza vilivyokuwa na soko la kulindwa katika nchi kama Uhindi kwa sababu serikali ya kikoloni ilidai kodi kali kwa bidhaa zisizotoka Uingereza."
] | 35
|
Je,twiga hubeba uja uzito kwa miezi ngapi?
|
[
"Twiga\nTwiga hubeba mimba kwa siku 400 mpaka 460 ambapo mara nyingi huzaa ndama mmoja hatimaye japo mapacha hutokea mara kadhaa. Mama hujifungua akiwa amesimama na kende lake hukatika mtoto aangukapo ardhini. Ndama akizaliwa huwa na urefu wa mita 1.8. Baada ya masaa kadhaa, mama huweza kukimbia japo ndani ya wiki mbili za mwanzo ndama hutumia muda mwingi kujilaza chini huku akilindwa na mama yake. Ndama huyo huwa hatamaniwi kuwindwa na simba, chui, fisi au mbwa mwitu. Ni asilimia 25–50 tu ya twiga ndiyo hufikia kuwa wakubwa. Twiga hukadiriwa kuishi miaka 20–25 mwituni na miaka 28 wakifugwa nje ya mbuga."
] |
[
"Wamatengo\nKipindi za uzazi mke hujitenga na mumewe kitendo kinachojulikana kama masegati kwa lugha ya Kimatengo. Mtoto anapofikisha miezi sita hupewa uji maarufu kama ukoba ambao hutengenezwa kwa unga wa ulezi na kinywaji kiiwatcho nimbi ambacho ni togwa ya watoto wachanga. Mtoto akishaanza kula vyakula tofauti ndipo mama yake huruhusiwa kuendelea kukaa chumba kimoja na mumewe.",
"Shinikizo la juu la damu\nShinikizo juu la damu hutokea takriban 8-10% za ujauzito. Wanawake karibu wote wenye shinikizo juu la damu wakiwa na mimba walikwishaumwa na shinikizio la damu la kawaida. Hali hiyo ikitokea katika ujaa uzito ni dalili ya kwanza ya kifafa cha mimba kabla hakijashikika kabisa. Maradhi hayo hutokea katika muda wa pili wa ujaa uzito na majuma machache baada ya kujifungua. Uaguzi wa maradhi hayo ni pamoja na shinikizo la damu kuongezeka na dalili za protini ndani ya mkojo. Maradhi hayo hutokea takribin 5% ya ujaa uzito yakisababisha takribin 16% ya vifo vya wenye ujaa uzito. Hatari ya kifo cha mtoto inaongezeka maradufu kutokana na maradhi hayo dunia nzima. Kwa kawaida hakuna dalili maalum za kifafa cha mimba kabla hakijashikika kabisa hugunduliwa na uchujaji wa kawaida. Zinapotokea dalili za maradhi hayo hizo ndizo ni kuumwa kichwani, taabu za kuona vizuri (mwanga wa kumulika ghafla) kutapika, maumivu ya epigastriumu na kuvimba. Kifafaa cha mimba kabla hakijashikika kabisa wakati mwingine inaweza kuletea hali inayotisha maisha inayoitwa kifafa cha mimba. Kifafa cha mimba kinaleta hali ya dharura ya shinikizo la damu inayotatiza sana. Matatizo hayo ni pamoja na upofu, kuvimba kwa ubongo, utendaji wa kiklonasi ulio katika hali ya kukazika au kuvutika na kutia kifafa, kuharibika kwa mafigo, edema ya mapafu, disseminated intravascular coagulation (kutoganda vizuri kwa damu).\nShinikizo juu ya damu ikiathiri uja uzito: Dawa Ukunga na Elimuuzazi:",
"Wagogo\nTembe huezekwa kwa udongo ambao hushikiliwa na miti midogomidogo iitwayo \"walo\". Walo huwa inashikiliwa na miti mikubwa kidogo iitwayo \"mahapa\" na mahapa hushikiliwa na miti mikubwa iitwayo \"michichi\". Michichi ambayo ndiyo hubeba uzito wote hushikiliwa na nguzo kubwa za miti imara na migumu. Nguzo hizo hutiwa \"masumbilili\".",
"Ondoa Giza Kitaa\nNari anaona watu wana mawazo ya kijinga kiasi kwamba hata lililo mbele yao wanashindwa kuliona. Anarejea maneno ya \"Macho Ngumu Kuona\". Uwoga katika maisha haukufanyi kufanikiwa bali kukudumaza. Sio kwamba ukiwa muoga ndio utaenda peponi. Namna ya ufundishaji ambao sio rafiki kwa wasomeshwaji. Watu hawaelewi kitu. Bado kuna wengine wanajifanya watumikia hip hop kumbe ndio wanafiki wakubwa katika suala zima la kuiponda. Wanashangazwa pamoja na majungu yao ndio kwanza muziki unapaa. Wanabaki na maswali tu. Vilevile anarejea jinsi Kilimo Kwanza kilivyoshindwa kumsaidia mtu wa hali ya chini. Nari anachukizwa na marafiki bandia wanajiofanya wanaeneza upendo ilhali wanaeneza skendo.",
"Wasangu (Tanzania)\nSasa kuku mweusi hutafutwa (sehemu zingine mbuzi au kondoo hutafutwa kwaajili ya shughuli hizi). Mambo yote yakiwa tayari watu wote wanaohusika hjuenda mahali palipo patakatifu na kuanza kuomba mvua inyeshe. Kasisi mkuu huanza kusema maneno haya. \"Uposhele inguku ini tuhanzaje hwunzi hwilwipei invula itonye, iviyabo vihwone. Ingukuinj mulyarrje mwendi mwikwizyanajei abantu balalamiha baiga, \"Tukosile yenu? Invulayinyu Mhutima?\"Tulaba twalamba sana ngatukosile shimo vyanje. Ngazilipo zimo uvitilwe utuwozye we wewe dada pipo nahumo uhwinyi washimbilile. Tusubila wenewe ungulubi uwinji numo.\"",
"Tatu Chafu\nPunde anaingia Uswege (Faraji Mhando) mwenye hasira juu ya tukio lililotokea na kufeli. Anawatisha na kuwaasa wakiendelea na ujinga wao watadakwa na kupotea mazima. Baada ya maneno ya kashfa, Uswege ambaye anaonekana ndiye mratibu wa matukio kibao. Anawagusia kuhusu mchongo mpya wa kuiba kiboksi chenye pete katika duka moja la sonara kwa Mpemba. Uswege anawaambia wakifanikisha wasimtafute. Yeye anajua wapi pa kuwapata. Huko magetoni, vijana wanacheza gemu kwenye TV, ghafula Mbita anagonga lango kama ugomvi, Bambino anakurupuka kwenda kumwaga dawa za kulevya chooni. Bila kujua aliyegonga ni Mbita ambaye kaja kununua bangi kwa Rochi. Kwa kigugumizi Bambino anasema kamwaga mzigo wa mzee Mangele.",
"Wahehe\nWajerumani wakati huo walikuwa na mashaka kwamba watawala wa Kiafrika, hususan Mkwawa, walikuwa wameanza kuonyesha upinzani wa wazi, hasa Mtemi Isike wa Tabora na Mbunga wa Ungoni ambao himaya zao zilipakana na Uhehe. Chifu mmoja wa Usagara aliwahi kutamka wazi, “Watu hawa (Wahehe) ndio pekee walioweza kuoga mchanga wa damu ya Mzungu ambao ‘bomba zao za moto’ ziliwafanya wengi washindwe kujitetea. Na kweli, vijiji vingi vilivyokuwa jirani na boma la Wajerumani viliendelea kutoa msaada kwa Mkwawa na Himaya yote ya Uhehe mpaka pale Kalenga ilipoangushwa.",
"Ondoa Giza Kitaa\nMwanzo tu mshangao wa baba kumkataa mtoto wake. Ugumu wa maisha uliopelekea dada zete kujiuza. Ukiangalia kwa kina Sir Elly anaona ugumu wa maisha sio kisingizio cha kufanya uhasherati kwa kujipatia kipato. Wangapi hawafanyi hayo na maisha yanaenda. Dhahiri kiza kimetanda ndio maana anasema ondoa giza kitaa. Wapo wengine wanaojita mambo safi mtaani na kunata, punde wanashika mimba na nyodo zote zinaisha. Kwa aibu anaamua kuwa kimya na limimba lake alilotoswa. Mimba za utotoni zinazungumzwa humu, jambo la kusikitisha kuona jamii inayotuzunguka inatazama jinsi wasichana wadogo wanavyodhalilishwa kwa kuzaa katika umri mdogo. Uzazi wa umri mdogo unachangamoto nyingi sana. Lakini juhudi za dhati hazijafanyika. Sir Elly anaona hili ni jukumu la kila mwanajamii kusimamia watoto wetu mtaani. Mtoto wa mwenzako ndio wako. Anaona siku hizi watoto wadogo si wadogo tena. Watoto wadogo wana mambo ya kikubwa hakuna mfano. Mtoto mdogo ana maovu rundo. Unatumwa ujumbe uwafikie watu wote wanaojiona wakubwa kuliko wenzao. Suala la kuuza ngada linaendelea kama kawaida, japo kunaonekana juhudi za kisiasa katika kusimamia suala hili. Huduma bado inapatikana licha ya mikwara mingi kuchimbwa. Sir Elly anaona ukiwachana kwa njia ya sanaa itasaidia kueneza habari za ukatazo dhidi ya usambazaji wa dawa za kulevya. Halafu Sir Elly anaitikia kwa kusema:",
"Hewa\nHewa ina uzito wake. Kwenye uwiano wa bahari kila mita ya mjao huwa na uzito wa kilogramu 1,2041 kg. Kwa sababu angahewa inafikia kilomita mamia juu ya uso wa dunia kuna uzito wa tani 10 au kilogramu 10.000. Huu ni uzitoa tunaobeba kila siku lakini hatuusikii kwa sababu kwetu ni kawaida na tunaihitaji. Kama tungeondoka kutoka eropleni bila kinga katika kimo kikubwa sana kama juu ya kilomita 50 tungekufa haraka sana si tu kwa sababu huko hakuna hewa ya kutosha kwa kupumua lakini kwa sababu uhaba wa kanieneo ungesababisha damu yetu kuchemka.",
"Ondoa Giza Kitaa\nPrime anaona ukubwani hakuna rafiki wa kudumu, na mwisho wa siku kila mtu lazima arudi kwa Mola wake. Maisha ni kupanda na kushuka, kufanikiwa au kutofanikiwa. Lakini mafanikio yako isiwe sababu ya wewe kujifanya hunijui au kunikana. Mwisho wa siku sote njia yetu ni moja. Tuishi kwa upendo. Prime anaona ulimwengu umebadilika sana. Mambo machafu yamekuwa kawaida katika jamii iliyotuzunguka. Wizi, ulaghai utapeli na kadhalika. Ubinadamu umepungua kiasi kwamba hata unasikia mlio wa bunduki hushituki tena. Unaona kawaida hata kama kuna mtu kauawa katika mlio huo. Anasikitishwa namna watu wanavyopandikiziana chuki kwa manufaa binafsi. Analitoa la moyoni kila mja alisikie. Anato fumbuzi kwa wale wenye vijiba vya nafsi kwa wenzao. Anatumia misamiati ya kuficha maneno makali katika sanaa. Jinsi wakubwa wanavyoonea wadogo kwa kutumia nyadhifa zao. Walio juu kuwaona walio chini hawana akili. Rejea mstari kama:"
] | 55
|
Nchi ya Urusi iko na ukubwa wa kiasi gani?
|
[
"Jiografia ya Urusi\nJiografia ya Urusi inaeleza tabia za nchi ya Urusi inayotanda juu ya maeneo mapana ya Eurasia ya kaskazini na ambayo ni nchi yenye eneo kubwa duniani, ikiwa na kilomita za mraba milioni 17.\nIna asilimia 11 za maeneo yote ya nchi kavu duniani ndani yake ambayo ni sawa na jumla ya maeneo ya Ulaya na Australia.",
"Urusi\nKwa eneo ni nchi kubwa kuliko zote duniani, ikiwa na km² 17,075,400.\nUrusi imepakana na Norway, Ufini, Estonia, Latvia, Lithuania, Poland, Belarus, Ukraine, Georgia, Azerbaijan, Kazakhstan, China, Mongolia na Korea ya Kaskazini."
] |
[
"Urusi\nTabianchi ya Urusi ni hasa ya kibara, kutokana na umbo la nchi na umbali wa sehemu nyingi na bahari. Maeneo mengi yana umbali wa kilomita 400 na zaidi kutoka ufukoni, na kitovu cha nchi kina umbali wa kilomita 3,840 kutoka bahari.",
"Gesi asilia\nMnamo mwaka 2004 takriban mita za mjao bilioni 589 zilizalishwa. Zilitosheleza asilimia 24 za mahitaji ya nishati duniani. Nchi zinazozalisha gesi nyingi duniani kwa sasa ni Urusi na Marekani. Urusi ina pia akiba kubwa duniani maana hapa kuna bado kiasi kikubwa sana ya gesi chini ya ardhi. Lakini nyingine zenye akiba kubwa ni nchi zilizopo kando la Ghuba la Uajemi ambazo ni Uajemi, Qatar, Saudia na Falme za Kiarabu.",
"Urusi\nKwa jumla kuna mito elfu kadhaa. Mingi iko sehemu ya beseni ya utiririshaji ya Bahari Aktiki ambako kuna watu wachache. Kwa hiyo sehemu kubwa ya maji haina matumizi kwa manufaa ya binadamu. Kinyume chake maeneo ya Urusi ya kusini kwenye vipindi vya joto na wakazi wengi yanaona vipindi vya uhaba wa maji kama vile beseni za mto Don na mto Kuban.",
"Jiografia ya Urusi\nZaidi ya hayo Urusi ina safu za milima mirefu hasa upande wa kusini na upande mashariki inayozuia kufika rahisi upepo kutoka Bahari Hindi na Pasifiki mwenye uweyo wa kupoza halijoto. Kinyume chake upepo kutoka Bahari aktiki unaweza kuingia bila vizuizi vya aina hii.",
"Jiografia ya Urusi\nTabianchi ya Urusi ni hasa ya kibara kutokana na umbo la nchi na umbali wa sehemu nyingi na bahari. Maeneo mengi yana umbalio wa kilomita 400 na zaidi kutoka ufukoni, na kitovu cha nchi kipo kwa umbali wa 3840 na bahari.",
"Urusi\nZaidi ya hayo Urusi ina safu za milima mirefu hasa upande wa kusini na upande wa mashariki ambazo zinazuia kufika kwa urahisi kutoka Bahari Hindi na Pasifiki upepo wenye uwezo wa kupoza halijoto. Kinyume chake upepo kutoka Bahari Aktiki unaweza kuingia bila vizuizi vya aina hii na kuleta baridi kali.",
"Njia ya reli\nUrusi na nchi zilizokuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti huwa na upana wa mita 1.520 ambayo ni pana zaidi kuliko nchi nyingi za jirani. Kwa sababu ya wingi wa usafiri wa reli ndani ya Urusi na nchi za Ulaya na China kuna vituo mbalimbali ambako sehemu ya chini za mabehewa zinabadilishwa kwa ajili ya upana husika wakati wa kuvuka mipaka.",
"Kiabaza\nKiabaza ni lugha ya Kikaukazi ya Kaskazini nchini Urusi na Uturuki inayozungumzwa na Waabaza. Mwaka wa 2010 idadi ya wasemaji wa Kiabaza nchini Urusi imehesabiwa kuwa watu 37,800. Pia kuna wasemaji 12,000 nchini Uturuki (2014). Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiabaza iko katika kundi la Abkhazi-Abazini.",
"Spitsbergen\nNchi nyingine zilijiunganisha na mkataba baadaye. Lakini ni Norwei na Urusi pekee ambazo zina shughuli kwenye visiwa hivi. Wakati wa Umoja wa Kisovyeti walikuwepo Warusi wengi waliochimba makaa na madini mengine lakini migodi yote haileti faida tena, imefungwa kwa kiasi kikubwa.",
"Jiografia ya Urusi\nSehemu kubwa ya mipaka ya nje iko kwenye maji. Pwani ndefu ni pwani ya kaskazini iliyopo ng'ambo ya Mzingo Aktiki; kwa hiyo pwani hiyo inafunikwa na barafu ya bahari kwa sehemu kubwa ya mwaka isipokuwa bandari ya Murmansk inayopokea maji fufutende kiasi kutoka mkondo wa ghuba. Bahari Aktiki, Atlantiki na Pasifiki zinagusana pwani za Urusi."
] | 60
|
Nani mmiliki wa kampuni ya google?
|
[
"Google\nMatumizi ya Google ni bure, lakini kampuni ina mapato makubwa kutokana na matangazo ya biashara kwenye kurasa zake na thamani ya kampuni imekadiriwa kuwa bilioni za dolar 130 hivi. Umaarufu wa mashine ya kutafuta ya Google umetokana na sababu mbalimbali ikiwemo kanuni zinazotumika kuzipa ukurasa daraja la mtandaoni kwa kutumia mfumo uliopewa jina la \"PageRank\" kutokana na jina la mmoja wa waanzilishi wa Google, Larry Page. watangazaji wengi hujitahidi kutumia mbinu mbalimbali ili kuwa na daraja la juu kwenye mashine yake ya kutafuta.",
"Google\nTovuti ni mali ya kampuni Google Inc. ya Marekani, lakini kampuni mama ni Alphabet Inc.. Kampuni ilianzishwa na Larry Page and Sergey Brin mwaka 1998, wakati walipokuwa wanafunzi wa chuo kikuu."
] |
[
"Nani\nNani alifunga katika dakika ya 10 katika FA Community Shield mwaka wa 2009, lakini United ilipoteza mechi hiyo kupitia mikwaju ya penalti kufuatia sare ya 2-2. Nani alijeruhiwa begani wakati wa mechi hiyo, ambayo awali ilitarajiwa kumweka hadi mwanzo wa msimu, lakini alipona na kuichezea Ureno dakika 17 dhidi ya Liechtenstein tarehe 12 Agosti, na kuanza mechi dhidi ya Birmingham City tarehe 16 Agosti. Ingawa aliandaa pasi lililomsababisha Wayne Rooney kufunga bao la ushindi katika dakika ya 34, Ryan Giggs aliingia kama mbadala wake baada ya nusu ya kwanza ya mechi. ] Kuondoka kwa Cristiano Ronaldo kwenda Real Madrid kulimaanisha kuwa kungekuwa na wachezaji wengi ambao wangetaka kuchukua majukumu ya “free-kick” na Nani alichapa na kufunga bao lake la kwanza la msimu wa 2009-10 kutoka kwa “free-kick” dhidi ya Wigan athletic, katika ushindi wa 5-0 ugenini.",
"Nani\nMechi ya kwanza ya Nani ya ligi kuu ya Uingereza ilikuwa katika mechi ya ufunguzi ya nyumbani, Manchester United ikiwa mwenyeji wa Reading tarehe 12 Agosti na Nani aliingia kama mbadala kwa Wayne Rooney, ambaye alipata jeraha la mguu. Manmo 26 Agosti 2007, Nani alifunga bao lake la kwanza la ushindani la Manchester United, bao la ushindi kutoka yadi 30 katika dakika ya 69 dhidi ya Tottenham Hotspur. Pia Nani aliandaa mabao muhimu kwa Louis Saha na Nemanja Vidic na kuruhusu Manchester United kuzicharaza Everton na Sunderland 1-0. Pia alifunga bao maarufu dhidi ya Middlesbrough, ambayo ilianzisha ushindi wa 4-1. Hii ilikuwa mechi ya kwanza ambayo ilidhaniwa kwamba Wayne Rooney na Carlos Tevez walionyesha ahadi ya kwanza ya kweli ya kufomu ushirikiano mzuri. Alirudi kwa klabu yake ya zamani, Sporting, katika mechi ya ligi ya Mabingwa barani Ulaya mwezi wa Septemba, ingawa ilikuwa mwenzake na mchezaji wa zamani wa Sporting Cristiano Ronaldo ambaye alifunga bao la ushindi katika ushindi wa 1-0.\nMnamo 16 Februari 2008, Nani alikuwa mchezaji bora katika mechi dhidi ya Arsenal katika raundi ya nne Kombe la FA, bao lake na pasi mbili alizoziandaa zilizosababisha mabao ziliisaidia United kushinda mechi hiyo 4-0 dhidi ya wapinzani wao jadi. Katika mechi hiyo, Nani alihusika katika ubishi pamoja na nahodha William Gallas wa Arsenal ambaye aliona kwamba Mreno alikuwa \"anamadharau\". Baada ya mechi, pia Arsène Wenger hakuwa amefurahishwa na kitendo cha Nani huku Gilberto Silva akisema kuwa Nani alikuwa na \"kuchwa kubwa (ujeuri)\".",
"Mara GROUP\nMara GROUP ni kikundi cha Kenya chenye kupigania mazingira ambacho kinalenga kuboresha utalii nchini Kenya. Lengo lake kuu ni kutoa msaada kwa jumuiya za kijamii kupitia Utumiaji na kuwaleta wafanyakazi wa kujitolea wa kimataifa ili kuboresha maisha ya wkakenya na hivyo kuchangia katika maendeleo ya jamii na mwingiliano wa kimila.\nKampuni ilianzishwa mwaka 2009 ikiwa na lengo la kukuza Kenya, kwa mfano wa kimataifa hasa baada ya ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya.\nMara ya Link hujihisisha na aina tatu za utalii, ambazo ni: Kujiburudisha, Biashara na hiari. Wao ni duka moja la mahitaji yote ya utalii. Huduma zao ni malazi, usafiri, ushauri (juu ya chanjo, masuala ya usalama, mahitaji ya usafiri mahitaji, kujitolea mipango ya misaada, na watu wengi zaidi), utalii mwelekeo na wengi zaidi.\nMashirika lengo kuu ni kurejesha sekta ya utalii, kulinda mazingira na ongezeko la joto duniani na kutetea amani kati ya watu wa Kenya.",
"John Cena\nJohn Felix Anthony Cena (/ siːnə /; aliyezaliwa Aprili 23, 1977) ni mchezaji wa mzuri wa miereka,mwimbaji, mwigizaji, na mmiliki wa televisheni Kwa sasa amesajiliwa WWE kampuni inayo wadhamini wacheza miereka, Cena alianza kazi yake ya kukabiliana na michezo wa miereka mwaka 1999 na Ultimate Pro Wrestlingiliyoko marekani (UPW) na alishinda michuano ya UPW Heavyweight mwaka uliofuata. Cena ali saini makubaliano ya maendeleo na Shirikisho la Wrestling World (WWF), baadaye limeitwa jina la World Wrestling Entertainment, au tu (WWE) mwaka 2001, kuanzia kwenye orodha kuu ya WWE mwaka 2002.",
"Party of National Unity (Kenya)\nPNU iliundwa haraka inaonekana bila maandalizi mazuri. Hadi mwanzo wa Septemba 2007 haikueleweka Kibaki atagombea urais kupitia chama gani. Chama cha NARC kilichokuwa chombo cha Kibaki mwaka 2002 ilikuwa mkononi mwa mwenyekiti wake Charity Ngilu asiyeonyesha dalili la kumwunga Kibako mkono. Wanasiasa wengi wa upande wa Kibaki waliwahi kuacha NARC na kujenga badala yake NARC-Kenya lakini kikundi hiki hakikujenga uhusiano mzuri na wanasiasa wa serikali ya umoja wa kitaifa walionekana kuwa muhimu kwa Kibaki kama vile Simon Nyachae wa FORD-Kenya au Njenga Karume wa KANU.",
"Aliko Dangote\nAliko Dangote (aliyezaliwa 10 Aprili 1957) ni mfanyabiashara nchini Nigeria. Yeye ni mmiliki wa Dangote Group, ambayo ina shughuli katika Nigeria na nchi nyingine kadhaa za Afrika Magharibi. Msaidizi tajiri wa Rais wa kitambo, Olusegun Obasanjo na chama tawala cha People's Democratic Party (PDP), Dangote huendesha biashara ya bidhaa ya Nigeria kupitia kampuni yake na kujuana na wanasiasa. Akiwa na wastani wa thamani wa karibu dola bilioni 2.5, alihesabiwa na Forbes kama mmoja wa watu wenye asili ya kiafrica tajiri kabisa, nyuma ya Mohammed Al Amoudi (bilioni $ 9,0 ) na Oprah Winfrey (bilioni $ 2,7).",
"Kampuni ya G.R. Kinney\nKampuni ya GR Kinney ilikuwa kampuni ya uzalishaji na uuzaji wa viatu kutoka mwaka wa 1984 hadi mwezi wa 16 Septemba,1998. Alama yake ya KNN katika orodha ya kampuni katika Soko la Hisa la New York ilianza kutumika Machi 1923.\nWazo la kutengeneza viatu lilianzishwa na George Romanta Kinney ambaye baba yake aliendesha duka la kuuza vitu vyovyote kwa jumla katika eneo la Candor, New York. Baba yake akapatwa na mzigo mkubwa wa madeni na George aliapa kulipa madeni hayo yote katika siku zake za baadaye. Katika mwaka wa 1894, akiwa umri wa miaka 28, kiwango cha pesa alizokuwa akiweka kando kilitosha kununua duka la Lester huko Waverly,New York. Mafanikio ya Kinney yaliletwa na kuuza viatu kwa bei nafuu kwa raia wafanyikazi wa Marekani.",
"Kuuza na kununua Hisa (Kenya)\nUnapotaka kununua hisa, wafaa kueleza broka wako ni hisa za kampuni gani wataka kununua, wataka kuzinunua kwa bei gani kila hisa na wataka hisa ngapi. Baada ya kumpa mwelekezo huu, broka wako atatafuta anaye hisa unazohitajikatika bei ulilotaja au la chini zaidina kisha, atazinunua chini ya jina yako.\nUbadilishanaji huu wa fedha na hisa utarekodiwa katika CDSC huku hisa ulizonunua zikiwekwa chini ya akaunti yako ya CDSC na zikiondolewa kutoka kwa akaunti ya mmiliki wa hapo awali.",
"Jabir Johnson\n\"Jabir Johnson \"Jaizmela\" Mkingimle\"' (alizaliwa 17 Agosti 1984, Kibena katika mkoa wa Njombe) ni mwandishi wa habari na mtangazaji nchini Tanzania. Machi 1, 2017 alisaini mkataba wa miaka miwili ambao ulipaswa kumalizika Februari 28, 2019 na kampuni ya Mpakasi Limited inayomiliki wavuti ya Hivisasa ambako amejikita katika masuala ya habari za michezo. Lakini ilipofika Desemba 12, 2017 mmiliki wa wavuti hiyo alitangaza kuifunga kutokana na changamoto lukuki alizokuwa nazo. Kabla ya hapo alikuwa akijitolea Sahara Media Group baada ya kumaliza mkataba wake na Gazeti la Tanzania Daima alilodumu nalo kwa miaka mitatu hadi Oktoba 28, 2016. Amekuwa akisikika katika studio za redio Kiss FM nchini Tanzania katika taarifa za habari, matukio na michezo."
] | 2
|
Je,Vita vya kwanza vya dunia viliisha mwaka gani?
|
[
"Ukristo barani Afrika\nVita vikuu vya dunia vilisaidia kukomaa kwa Kanisa la Afrika. Kwa mfano, mahali pengi Tanzania makanisa yalianzishwa na wamisionari Wajerumani (Wakatoliki, Walutheri, Wamoravia, Wasabato n.k.). Katika vita vikuu vya kwanza (miaka 1914-18) jeshi la Kiingereza liliingia na kuteka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani (baadaye Tanganyika, Rwanda na Burundi). Raia wa Ujerumani walifukuzwa pamoja na wamisionari.",
"Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia\nVita Kuu ya Kwanza ya Dunia ilikuwa vita iliyopigwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918. Mataifa wapiganaji yalikuwa Ujerumani, Austria-Hungaria, Bulgaria na Uturuki (ziliitwa \"Mataifa ya Kati\", ing. \"central powers\") kwa upande mmoja dhidi ya Ufaransa, Urusi, Uingereza, Italia, Marekani na nchi mbalimbali zilizoshirikiana nazo (zilitwa \"Mataifa ya Ushirikiano\", ing. \"allied powers\")."
] |
[
"Pikipiki\nVita vya kwanza vya dunia vilichangia pakubwa katika uboreshaji wa pikipiki. Wanajeshi waliona kuwa walikuwa wakitumia muda mrefu sana kusafiri kwa miguu au farasi na kwa hiyo, mahitaji ya pikipiki yakaweza mengi. Kampuni ya Harley-Davidson ilijipata ikitumia takribani asilimia hamsini ya wakati wake katika kutengeneza pikipiki za wanajeshi waliokuwa kwenye vita.",
"Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia\nIlikuwa pia vita ya kwanza iliyopigwa kote duniani ilhali habari zake ziliweza kufika katika muda wa masaa au siku chache kwa mataifa yote kutokana na upatikanaji wa vyombo vya mawasiliano hasa simu za kimataifa na redio.",
"Vita baridi\nVita baridi vilianza baada ya vita kuu ya pili ya dunia. Marekani, Uingereza na Ufaransa zilikuwa nchi washindi wa vita hii dhidi ya Ujerumani. Urusi ulikuwa na siasa ya kikomunisti lakini washindi wengine walifuata siasa ya kidemokrasia pamoja na uchumi wa kibepari. Ikumbukwe kuwa, Urusi ilijitoa kwenye vita vya kwanza vya dunia baada ya kufanya mapinduzi ya Kikomunisti mwaka 1917 hivyo kuachana na ushiriki wa vita hivyo vya mabepari.",
"Kalenda\nHesabu ya wiki haifuati kalenda ni kipindi cha siku 7 kinachorudia mfululizo bila kujali mwisho au mwanzo wa mwaka. Asili yake iko katika Mashariki ya Kati hasa Babeli ikasambazwa kupitia imani ya Uyahudi na Ukristo. Inaanza kwa siku ya Jumapili inayotazamiwa kidini kama siku ya kwanza ya uumbaji wa dunia na kwa wakristo pia siku ya ufufuo wa Yesu unaotazamiwa kama uumbaji wa pili. Kwa kusudi la kupanga maisha na hasa kazi wiki za mwaka zinahesabiwa kuanzia 1 - 52; hapo wiki ya kwanza na wiki ya mwisho kwa kawaida si kamili kwa sababu siku kadhaa zimo katika mwaka uliotangulia au kufuata.",
"Nicolaus Copernicus\nCopernicus hakuwa mtu wa kwanza aliyewaza ya kwamba Dunia inazunguka Jua: miaka 2000 kabla yake wanafalsafa kadhaa wa Ugiriki waliwahi kufundisha hivyo. Lakini tangu maandiko ya Ptolemaio wataalamu wa nyota pamoja na walimu wa dini za Ukristo na Uislamu walikubaliana kwamba Dunia ni kitovu cha Dunia na Jua pamoja na sayari zote zinaizunguka. Kitabu cha Copernicus kilikuwa cha kwanza kilichoondoa Dunia katika kitovu cha Dunia na kwa ujumla alipingwa na wataalamu wengi.",
"Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania\nVita kubwa inayojulikana zaidi ilikuwa Vita ya Uganda na Tanzania kwenye miaka ya 1978–1979. Ilianza wakati wa utawala wa dikteta Idi Amin na uvamizi wa jeshi la Uganda katika Mkoa wa Kagera wa Tanzania tarehe 25 Oktoba 1978. Katika muda wa wiki chache Tanzania ilipanusha idadi ya jeshi hadi kufikia 100,000 kwa kuingiza askari wa polisi, wa huduma ya magereza, kutoka Jeshi la Kujenga Taifa na wanamigambo, likisaidiwa na vikundi vya wapinzani wa Idi Amin. Katika Novemba jeshi la Tanzania lilianza kushambulia Wauganda. Hadi mwanzo wa Disemba 1978 Mkoa wa Kagera ulikuwa tena mkononi mwa Tanzania. Tarehe 21 Januari 1979 askari wa Tanzania walivuka mpaka wa Uganda, na tarehe 11 Aprili 1979 walivamia Kampala. Idi Amin alikimbia Libya na JWTZ ilibaki Uganda kwa muda hadi serikali mpya ya Uganda iliimarika.",
"Mkimbizi\nVita na migogoro ya kisiasa wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia ilisababisha kiasi kikubwa cha uhamisho wa lazima (angalia Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, ukombozi na kufukuzwa). Mnamo mwaka wa 1943, Muungano wa nchi Rafiki uliunda Shirika la Umoja wa Mataifa la Msaada na Kuanzisha Maisha Mapya (UNRRA kwa lugha ya Kiingereza) ili kutoa misaada kwa maeneo yaliyokombolewa kutoka nguvu za Kiaksisi, ikiwemo maeneo ya Ulaya na Uchina. Juhudi hizi zilijumuisha kuwarudisha zaidi ya wakimbizi milioni saba, ambao wakati huo walijulikana kama watu waliofukuzwa kutoka makwao, hadi katika nchi zao za kiasili na kuanzisha makambi ya watu waliotimuliwa makwao ya wakimbizi milioni moja ambayo walikataa kurudishwa nyumbani.",
"Mto Marne\nMto Marne ulikuwa eneo la vita viwili wakati wa Vita vya Kwanza vya Dunia. Vita ya kwanza vilikuwa mgeuko wa Vita vya Kwanza vya Dunia World katika mwaka wa 1914. Vita vya pili vilipiganwa miaka minne baadaye, katika mwaka wa 1918.\nKatika karne ya 19 na 20, Marne ulipendeza wachoraji wasanii wengi miongoni mwao ni:",
"Greatest Hits (albamu ya Spice Girls)\nGreatest Hits ni mkusanyikao wa vibao vikali vya kundi la muziki wa pop la Kiingereza, Spice Girls. Na pia ndiyo albamu ya kwanza kutolewa baada ya miaka saba na ilisaidiwa na sindikizo la ziara yao ya kimataifa. Ilipata kutolewa moja kwa moja dunia kote mnamo mwezi wa Novemba katika mwaka wa 2007, kasoro Marekani pekee ambapo ilipata kutolewa mwisho 6 Novemba 2007 na kuja kutolewa ile kamili mnamo tar. 15 Januari 2008. \"Greatest Hits\" imeuza takriban nakala zaidi ya milioni 1.7 kwa hesabu ya dunia nzima.Mauoz ya IFPI:1,700,000"
] | 58
|
Nchi ya Msumbiji imepakana na nchi ngapi?
|
[
"Msumbiji\nMsumbiji iko ufukoni mwa Bahari Hindi ikipakana na Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Uswazi."
] |
[
"Msumbiji (kisiwa)\nKisiwa cha Msumbiji au kwa lugha ya Kireno \"Ilha de Moçambique\" ni kisiwa kidogo na pia mji kilichopo 3 km mbele ya mwambao wa Msumbiji ya kaskazini. Urefu ni 3 km na upana kati ya 500 hadi 200 m. Kisiwa ni sehemu ya mkoa wa Nampula. Mji huu ni chanzo cha koloni ya Kireno ya Msumbiji ilikuwa mji mkuu wa nchi kwa karne kadhaa.",
"Newala\nWilaya hii imepakana na Wilaya ya Masasi upande wa magharibi na kaskazini, wilaya ya Tandahimba upande wa mashariki na kaskazini, mto Ruvuma na Msumbiji kwa kusini. Newala imepakana kwa karibu kabisa na nchi ya Msumbiji ambapo mto Ruvuma ndio unaotenganisha wilaya ya Newala na nchi ya Msumbiji.",
"Tabianchi ya Tanzania\nTanzania ni nchi iliyopo mashariki mwa bara la Afrika na imepakana na nchi zifuatazo: upande wa kaskazini imepakana na nchi za Kenya na Uganda, upande wa magharibi imepakana na nchi za Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, upande wa kusini kuna nchi za Zambia, Malawi na Msumbiji wakati upande wa mashariki kuna Bahari ya Hindi.",
"Wilaya ya Nanyumbu\nInapakana na Mkoa wa Lindi upande wa Kaskazini, Mkoa wa Ruvuma upande wa Magharibi, Kwa upande wa Mashariki imepakana na Wilaya ya Masasi na Nchi ya Msumbiji kwa upande wa Kusini.\nWilaya ina jumla ya kata 14 na vijiji 89 mpaka sasa. Shughuli za kilimo ndio tegemeo kuu la wananchi wa wilaya hii.",
"Zambezi (mto)\nZambezi ni kati ya mito mirefu ya Afrika ikiwa na nafasi ya nne baada ya Nile, Kongo na Niger. Ni mto mrefu wa Afrika wa kuingia Bahari Hindi. Beseni lake lina km² 1,570,000 au nusu ya mto Nile. Chanzo chake iko Zambia inapita Angola mpakani na Namibia, Botswana, Zambia na Zimbabwe kwenda Msumbiji inapofikia Bahari Hindi katika delta ya 880 km².",
"Misri\nTabianchi ni yabisi sana na maeneo makubwa ni jangwa, pamoja na oasisi na maeneo ya savana ya miiba. Karibu wananchi wote huishi ndani ya kanda nyembamba ya bonde la mto Naili. Bonde hili linavuka nchi kuanzia mpakani na Sudani katika kusini kuelekea kaskazini hadi mdomo wa mto kwenye Bahari ya Mediteranea. Ardhi pande zote mbili za mto inamwagiliwa na kulimwa. Kwatika umbali mdogo kutoka mto jangwa inaanza.",
"Kusini\nUkitazama jua linapochomoza kusini huwa ni upande wa kulia. Kusini kawaida huwa chini zaidi kwenye ramani. Marekani ipo kusini mwa nchi ya Kanada, Tanzania ipo kusini mwa nchi ya Kenya, na Msumbiji ipo kusini mwa nchi ya Tanzania. Ncha ya kusini ni kusini ya mbali unayoweza kwenda.",
"Mpumalanga\nMpumalanga imepakana na Uswazi na Msumbiji halafu na majimbo ya KwaZulu-Natal, Dola Huru, Gauteng na Limpopo. Hifadhi ya Kruger ambayo ni hifadhi ya wanyama mashuhuri imo jimboni.",
"Mtwara Vijijini\nWilaya hii imepakana na Msumbiji upande wa kusini, Wilaya ya Tandahimba upande wa magharibi, Mkoa wa Lindi upande wa kaskazini na Mtwara Mjini pamoja na Bahari Hindi upande wa Mashariki.",
"Wilaya ya Mbinga\nWilaya hii imepakana na mkoa wa Iringa upande wa kaskazini, wilaya za Songea mjini na Songea vijijini upande wa mashariki, Msumbiji upande wa kusini na Ziwa Nyassa upande wa magharibi."
] | 43
|
Dini ya Kiislamu ina takriban watu wangapi?
|
[
"Uislamu\nWafuasi wa imani hiyo huitwa \"Waislamu\" na wanakadiriwa kuwa milioni 1,400 hivi. Hivyo ni dini ya pili duniani yenye wafuasi wengi baada ya Ukristo wenye wafuasi milioni 2,200."
] |
[
"Jamhuri ya Watu wa Zanzibar\nDini ya Uislamu ina kiasi cha 97% za wananchi wote. Waliobaki ni hasa Wahindu na Wakristo, lakini Wahindu wengi walikimbia nchi au kuuawa wakati wa mapinduzi ya mwaka 1964. Wakristo walikuja wakati wa utawala wa Kireno na ukoloni wa Uingereza.",
"Muhinda\nDini kuu ni mbili, Ukristo na Uislamu, nazo zinamwabudu Mwumba wa mbingu na dunia, Mungu wa kweli wa wanadamu wote. Ukristo ndio wenye asilimia kubwa, kwani kuna Ukatoliki, Anglikana, Sabato, Pentekoste (PAG, TAG, EAGT, PEFA, FPTC), Moravian n.k. Kata ina kanisa kubwa la Katoliki la Mt. Maria Mlango wa Mbingu tangu mwaka 1946. Uislamu una Wasuni, Washia na Wahabia.",
"Dini nchini Tanzania\nLakini ni wazi ya kwamba dadi ya wafuasi wa dini za jadi imeendelea kupungua. Baadhi ya viongozi na wanaelimu-jamii wanakadiria kwamba jumuia za Kikristo na Kiislamu zipo sawa tu kwa ukubwa, zote huhesabiwa kiasi cha asilimia 30 hadi 40 kwa idadi ya wakazi, na waliosalia ni waumini wa imani zingine, dini za jadi, na wale wasio na dini kabisa.",
"Uislamu katika Guinea ya Ikweta\nKwa mujibu wa Ripoti ya 2006 ya Kitengo cha Uhuru wa Dini cha Kimataifa cha Marekani, waumini wa dini ya Kiislamu wapo chini ya asilimia moja idadi ya wakazi wote wa nchi ya Guinea ya Ikweta. Ripoti ya wavuti ya Adherents.com, hata hivyo, imekadiria ya kwamba Waislamu wameongezeka kutoka asilimia 1 hadi asilimia 25% ya jumla ya wakazi wote wa nchini hiyo. Wahindi walio wengi nchini humo ni Waislamu. Kuna msikiti mmoja wa Ahmadiyya nchini humo.",
"Falme za Kiarabu\nUislamu ndio dini ya wenyeji (85% Wasuni na 15% Washia) na dini rasmi ya nchi, lakini kuna uhuru wa dini kwa wote, isipokuwa si uhuru wa kuieneza kwa wengine. Kati ya wakazi wote, Waislamu ni 76-77%, Wakristo (hasa Wakatoliki) ni 9-12%, Wahindu ni 4%, Wabuddha 2%, n.k.",
"Uislamu nchini Swaziland\nTaifa la Swaziland ni nyumbani pa watu wanaozidi milioni 1, ambao asilimia 10 wanakadiriwa kutambuliwa kama Waislamu kwa mujibu wa CIA, ambao wengi wao ni wafuasi wa dhehebu la Sunni. Uislamu nchini Swaziland huenda unatoka mbali tangu enzi za ukoloni, wakati huo Swiziland ilikuwa jirani mno na Afrika Kusini, Waislamu wengi waliloea nchini humo wakitokea nchi nyingine chini ya utawala wa Dola la Uingereza. The Jumuiya ya Kiislamu ya Ahmadiyya inadai ina wafuasi wapatao 250 nchini humo.",
"Fiji\nDini ni moja ya mambo ambayo hutofautisha jamii mbalimbali katika visiwa vya Fiji, hususani baina ya makabila ya Wafiji wenyewe na Wahindi waishio Fiji, ambapo asilimia kubwa ya wenyeji ni Wakristo, wakati watu kutoka India ni Wahindu (70%) na halikadhalika Waislamu (17.9%).",
"Mngazi\nUpande wa dini, wakazi wa kata ya Mngazi wamegawanyika katika makundi makubwa mawili: Wakristo na Waislamu. Wakristo wengi ni Wakatoliki na wachache Wapentekoste wa kanisa la TAG ambao wengi wao ni wahamiaji.",
"Ndembezi\nWakazi wengi wa kata hii ni Wanyamwezi, na Wasukuma, pia kuna makabila ya Wanyiramba, Wanyaturu na Waarabu wachache. Wenyeji wa kata hii ni Waumini wa Dini ya Kikristo, Kiislaamu na dini za kienyeji. Kuna misikiti mitatu, makanisa tisa ya madhehebu tofauti ya kikristo na maeneo matatu ya matambiko ya dini za kienyeji yajulikanayo kama Mazimbo. Wenyeji wa Ndembezi ni wakarimu sana ambapo katika kipindi cha mavuno hupenda kubadilishana zawadi za mavuno hasa maboga, karanga, kunde na mboga za majani aina ya mlenda, mswalu, na mgagani. Chakula kikuu cha wakazi wa kata hii ni Ugali ukiambatana na mboga tofauti tofauti kama vile dagaa, nyama, kisamvu, mlenda, na mboga nyinginezo zinazopendelewa mkoani Tabora. Mara baada ya msimu wa mavuno kwisha, wakazi wa kata hii huingia katika msimu wa burudani kuanzia mwezi juni hadi septemba ambapo burudani kuu huwa ngoma za jadi maarufu kwa jina la Pubha(BENI) na HIYALI. Ngoma hizi hushirikisha pande mbili pinzani ambapo kila upande huimba na kucheza huku Manju wao akifanya michezo mbalimbali juu ya uchanja ili kuvutia watazamaji upande wake. Pande hizi pinzani huitwa Wazubha na Wagika wakati mwengine pia hushirikisha ngoma ya tatu ijulikanayo kama Wayeye. Upande utakaovutia watu wengi ndio huwa washindi.",
"Indonesia\nIdadi kubwa ya wakazi (87.2 %) wanahesabiwa kuwa Waislamu (karibu wote Wasuni), 9.8 % kama Wakristo (Waprotestanti 6.9 %, Wakatoliki 2.9 %), 1.6 % Wahindu na 0.7 % Wabuddha. Wahindu wako hasa kwenye kisiwa cha Bali. Hizo zote ni dini zilizotambulika rasmi pamoja na ile ya Konfusio (0.05 %)."
] | 7
|
Je,Michael Wamalwa Kijana alikuwa katika chama gani ya kisiasa?
|
[
"Michael Wamalwa Kijana\nKatika pilikapilika za uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi katika Kenya huru wa mwaka wa 1992, Wamalwa alijitambulisha na FORD-Kenya, chama ambacho kilijiondoa kwenye muungano wa upinzani wa FORD. Alichaguliwa kuwa mbunge wa eneo bunge la Saboti na vilevile Makamu Mwenyekiti kwanza wa chama chake. Mnamo Januari 1994, akawa mwenyekiti wa FORD-Kenya kufuatia kifo cha Oginga Odinga. Aligombea uchaguzi wa Kenya wa mwaka wa 1997 kama kiongozi wa upinzani lakini hakufanya vyema na alikuja wa nne katika idadi ya kura za kitaifa."
] |
[
"Michael Wamalwa Kijana\nKatika pilkapilka za uchaguzi wa mwaka 2002, walianzisha muungano wa kisiasa na Mwai Kibaki na Charity Ngilu ili kuja na upande wa kushinda. Baadaye Kalonzo Musyoka na Raila Odinga,walipogundua upande wao wa KANU ulikuwa umeelekea kupoteza, walibadili mrengo na kujiunga nao ili kufaidi na hali na watu kwa sasa kutoa changamoto kwa chama cha aliyekuwa rais wakati huo Daniel arap Moi, Kenya African National Union, Kenya African National Union (KANU). Muungano huu uliitwa National Rainbow Coalition (NARC), na ulipata ushinda mkubwa katika uchaguzi huo na Mwai Kibaki kama Rais. Wamalwa aliteuliwa makamu wa rais.",
"Michael Wamalwa Kijana\nMwisho mwisho wa mwaka wa 2002, wakati wa kampeni za uchaguzi, Mwai Kibaki alijeruhiwa vibaya sana katika ajali ya gari na alipelekwa London kwa matibabu. Aki huko,alitembelewa na Wamalwa ambaye pia aliugua na ilibidi atibiwe kwa matatizo ya figo. Hii ilikuwa dalili ya ugonjwa zaidi kwani alikuwa mgonjwa tena katikati ya mwaka wa 2003 na kwa mara nyingine tena, alitibiwa London. Alipata nafuu kidogo na alirejea Kenya kuoa Yvonne Nambia, katika sherehe kuu.Ilisemekana kuwa yeye alioposa kwa Kiingereza cha siku za Shakespea na aliwasili kanisa katika Vintage Ford akiwa amevalia kanzu.",
"Michael Wamalwa Kijana\nKuingia kwake siasa nchini Kenya kulikuja katika uchaguzi wa ubunge wa 1974. Akiwa tu na umri wa miaka 30, wapinzani wake walimpuzilia yeye kama kijana na pia kutoka familia ya kitajiri mno ili kuwakilisha eneo bunge lake vyema. Kampeni yake ilikuwa ya kifahari: ilijumuisha matumizi ya ndege na mikutano ya kampeni za umma iliyoja ufujaji wa pesa. Hatimaye alishinda kiti cha mwaka 1979, kwa kushirikiana na Masinde Muliro.",
"Michael Wamalwa Kijana\nAlikuwa mbunge wa eneo bunge la Saboti katika wilaya ya Trans-Nzoia, mkoa wa Rift Valley. Mji wake wa nyumbani ulikuwa Kitale.\nLabda ni yeye wa kipekee katika historia ya Kenya aliyeweza kupata kura bila misingi ya kikabila.",
"Michael Wamalwa Kijana\nMichael Wamalwa Kijana (25 Novemba 1944 - 23 Agosti 2003) alikuwa mwanasiasa nchini Kenya na wakati wa mauti yake, alikuwa Makamu wa Rais wa Kenya.",
"Michael Wamalwa Kijana\nAlirejea Kenya mwaka huohuo na kuanza kufundisha sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi. Baadhi ya wanafunzi aliofundisha walikuja wakawa washirika na wapinzani wake wa kisiasa baadaye. Katika kipindi hiki, alisimamia mashamba ya familia katika eneo la Kitale na vilevile kushikilia nyadhifa kadhaa maarufu serikalini ikiwa ni pamoja na meneja mkuu wa Kenya Stone Mining Company na mkurugenzi wa Kenya-Japan Association.",
"Michael Wamalwa Kijana\nChristopher Michael Kijana Wamalwa alizaliwa Sosio, kijiji kilichoko karibu na Kimilili, katika wilaya ya Bungoma nchini Kenya. Alikuwa mwana wa mbunge mashuhuri, William Wamalwa.",
"Michael Wamalwa Kijana\nSambamba na Tom Mboya, Ronald Ngala na PLO Lumumba, alikuwa na kipawa cha unenaji.",
"Michael Wamalwa Kijana\nMiezi miwili tu baada ya harusi, Wamalwa alirudi katika hospitali ya Royal Free Hospital kwa uchunguzi na kupelekea kuenea uvumi kwamba afya yake ilikuwa mbaya zaidi kuliko madaktari walivokuwa wakidhani."
] | 0
|
Eneo la Uajemi lina ukubwa gani?
|
[
"Ghuba ya Uajemi\nEneo lote la ghuba ni 233,000 km². Maji matamu huingia kwa njia ya mito ya Frati na Hidekeli inayoungana katika Shatt al Arab."
] |
[
"Eneo Bunge la Embakasi\nEneo Bunge la Embakasi ni eneo bunge la uchaguzi nchini Kenya. Ni moja kati ya maeneo bunge nane katika Mkoa wa Nairobi. Linajumuisha vitongojo vya mashariki na kusini mashariki vya Nairobi. Ikiwa na wapiga kura waliosajiliwa takribani 164,227, ndilo eneo bunge lenye wapiga kura wengi sana nchini Kenya. Lina mipaka sawia na Taarafa ya Embakasi. Eneo lote la eneo bunge hili liko katika eneo la Baraza la Jiji la Nairobi. Lina ukubwa wa eneo wa kilomita mraba 208.",
"Eneo Bunge la Kasarani\nEneo Bunge la Kasarani ni eneo bunge le uchaguzi nchini Kenya. Ni mojawapo wa maeneo bunge nane katika Mkoa wa Nairobi. Linajumuisha maeneo ya kaskazini na kaskazini mashariki ya Nairobi. Eneo Bunge la Kasarani lina mipaka sawia na Taarafa ya Kasarani. Eneo lote la bunge hili liko katika eneo la Baraza la Mji wa Nairibi. Lina ukubwa wa eneo wa kilomita mraba 86. Lilikuwa linajulikana kama Eneo Bunge la Nairobi Northeast katika uchaguzi wa miaka za 1963 na 1969,na kama Eneo Bunge la Mathare katika uchaguzi wa kuanzia mwaka wa 1974 hadi uchaguzi mdogo wa mwaka wa 1994. Tangu uchaguzi wa 1997,limekuwa likijulikana kama Eneo Bunge la Kasarani.",
"Eneo Bunge la Dagoretti\nEneo Bunge la Dagoretti ni eneo bunge le uchaguzi nchini Kenya. Ni mojawapo wa maeneo bunge nane katika Mkoa wa Nairobi. Linajumuisha vitongoji vya magharibi vya Nairobi. Eneo Bunge la Dagoretti lina mipaka sawia na Taarafa ya Dagoretti ya Nairobi. Eneo lote la bunge hili liko katika eneo la Baraza la Mji wa Nairibi. Lina ukubwa wa eneo wa kilomita mraba 39 . Lilikuwa linajulikana kama Eneo Bunge la Nairobi West katika uchaguzi wa mwaka wa 1963 ,lakini jina lake lilibadilisdhwa hadi la sasa kuanzia uchaguzi wa 1969.",
"Marekani\nEneo la Marekani lina ukubwa wa kilometa mraba 9,826,675 na liko hasa katika bara la Amerika Kaskazini kati ya Kanada upande wa kaskazini na Meksiko upande wa kusini.",
"Eneo Bunge la Othaya\nEneo Bunge la Othaya ni eneo la uchaguzi nchini Kenya. Eneo Bunge la Othaya ni mojawapo wa maeneo bunge katika Wilaya ya Nyeri, Mkoa wa Kati. Eneo Bunge la Othaya lina jumuisha taarafa ya Othaya ya Wilaya ya Nyeri.\nEneo bungehili lilianzishwa kwa ajili ya uchaguzi wa 1988.",
"Wabondei\nKama marehemu alikua ameoa ama kuolewa Linaandaliwa tambiko la kimila ambalo linaitwa kucha au mkucha ambapo mtu anachuku jembe na kikapu kisha panakokwa moto, mtu Yule anakwenda kujificha akishajificha anagonga lile jembe kidogo kisha anasema “Mkucha mkucha” mwengine anaitikia “Eehee” Yule mtu anasema tena “Fulani kafa” (Kwa kulitaja jina la aliekufa) Yule muitikiaji anauliza “Kafa?” kisha “kaolewa/kaoa wakati gani?” Yule mtu anautaja ule wakati “Wakati Fulani” Muitikiaji anauliza tena “Mahali kalipa?” atajibiwa kuwa amelipa ama hajalipa kisha watauliza madeni yake ya ndoa tu na atauliza pia alioa wake wangapi atajibiwa katika mfumo huo huo, ana watoto wangapi.. atajibiwa baada ya ukucha kumalizika sasa inafuata Ngoma ya Tindia na kisha Ngoma ya ukaa",
"Henrie Mutuku\nAlbamu yake ya kwanza ilikuwa \"Simama\" (Stand) ambayo nyimbo kama \"Usichoke\" (akimshirikisha Roughtone na RK) na \"Manzi wa Maana\" (akimshirikisha KJ wa Redykulass-aKundi la waigazaji wacheshi la Kenyan). Pia amemshirikishwa katika vipindi vya redio katika vituo vya redio kadhaa maarufu kama Kiss 100 “Smirnoff Top 7 songs in Nairobi”, East Africa FM Radio ‘Link’ na Kampala FM as voted by listeners[7].",
"Eric Wainaina\nMwaka 2002, alicheza katika uzinduzi wa Mahakama ya Kimataifa katika Makao Makuu ya Umoja wa Kimataifa mjini New York, iliyosimamiwa na Kofi Annan. Amezuru Uswisi kwa miaka 4 mfululizo na kutumbuiza katika Festival Mundialhuko Uholanzi mwaka 2003. Mwaka huo alitumbuiza katika Harare International Festival of the Arts (HIFA). Baada ya sherehe alimkosoa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe; jambo lilofanya vyombo vya habari vya Zimbabwe kumwandikia manoni yasiyoridhisha. Mwaka 2004 alitumbuiza katika tamasha la Sauti za Busara Zanzibar, sherehe ya muziki ya Afrika Mashariki.",
"Lorna Laboso\nNdege hiyo iligonga nyumba katika soko la Kajong'a karibu na Nairagie Enkare, pale Enoosupukia, Wilaya ya Narok, karibu na Narok na Mbuga ya wanyama ya Masai Mara\nNdege iliyokuwa ikiwabeba ilikuwa imeondoka Uwanja wa Ndege wa Wilson mjini Nairobi;\nPia rubani wa ndege hiyo na mlinda Usalama walifariki.\nRais Mwai Kibaki alituma risala za rambirambi na kuamrisha kupeperushwa kwa bendera Nusu Mlingoti.\nWaziri Mkuu Raila Odinga ambaye ni Kinara wa ODM alisema pia kuwa ilikuwa hali ya huzuni sana.",
"Irene Uwoya\nUwoya alianza shule ya msingi Mlimwa kisha akahamia Shule ya Bunge iliyopo Dar-es-Salaam kwa ajili ya elimu ya upili, baadaye akaenda Greenville huko jijini Kampala, Uganda. Kwenye mwezi wa Oktoba, 2017, habari zilitapakaa katika mitandao mbalimbali nchini Tanzania kuwa Uwoya ameolewa na Dogo Janja - msanii wa hip-hop Tanzania. Siku kadhaa mbele kupitia ukurasa wake wa Instagram Uwoya alithibitisha kuolewa na Dogo Janja."
] | 60
|
Gabon ilipata uhuru mwaka gani?
|
[
"Gabon\nJamhuri ya Gabon, kutoka kushinda uhuru kutoka Ufaransa tarehe 17 Agosti 1960, imeongozwa na Rais watatu, Léon M'ba, El Hadj Omar Bongo ambaye amekuwa kiongozi kutoka mwaka wa 1967 hadi kifo chake (2009: ndiye aliyekuwa kiongozi barani Afrika aliyeshikilia uongozi kwa muda mrefu zaidi), halafu mwanae Ali.",
"Historia ya Gabon\nJamhuri ya Gabon, kutoka kushinda uhuru kutoka ukoloni wa Ufaransa tarehe 17 Agosti 1960, imeongozwa na Rais watatu, Léon M'ba, El Hadj Omar Bongo ambaye amekuwa kiongozi kutoka mwaka wa 1967 hadi kifo chake (2009: ndiye aliyekuwa kiongozi barani Afrika aliyeshikilia uongozi kwa muda mrefu zaidi), halafu mwanae Ali.\nMwaka wa 1990 Gabon ilianza demokrasia ya vyama vingi na katiba ya kidemokrasia ambayo inaruhusu ukweli wa uchaguzi na utekelezaji wa idara za serikali.",
"Libreville\nTangu 1866 ikawa makao makuu ya jimbo la Gabon. katika karne ya 20 ikawa bandari kuu ya Afrika ya Ikweta ya Kifaransa ikaendelea kukua polepole. Tangu uhuru wa Gabon mwaka 1960 imekuwa mji mkuu wa nchi hii.",
"Historia ya Afrika\nKatika mwaka wa 1960 Ufaransa ukatoa uhuru kwa Cameroon, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Congo (Brazzaville), Cote d'Ivoire, Dahomey (Benin), Gabon, Madagascar, Mali, Mauritania, Niger, Senegal na Volta ya Juu (Burkina Faso)."
] |
[
"Omar Bongo\nKiongozi huyo amevunja rekodi ya kuwa Rais aliyekaa muda mrefu marakani kuliko Rais yeyote barani Afrika. Rais huyo amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 73, ambapo ameiongoza Gabon kwa miaka 42.\nBongo alijiunga na serikali ya Gabon mwaka 1965 na mwaka 1967 akawa makamu wa Rais ambapo mwaka huo huo akashika hatamu ya kuwa Rais wa nchi hiyo kufuatia cha kifo cha ghafla cha Rais Leon Mba.\nBongo alipoingia madarakani alijenga utawala imara ambao ulinufaika zaidi baada ya kugunduliwa kwa mafuta nchini Gabon ingawa utajiri wake ulinufaisha idadi ndogo ya watu wanaokadiriwa kuwa milioni 1.5. kitu kilicholeta lawama kubwa kwa kiongozi huyo.\nRais huyo amefariki dunia wakati akipata tiba ya saratani jijini Barcelona nchini Hispania.\nRais Bongo ameaga dunia takribani miezi mitatu baada ya kifo cha mkewe, Edith Lucie Bongo Ondimba (45) aliyefariki dunia 14 Machi mwaka huu wakati akipata tiba mjini Rabat nchini Morocco.\nBongo na Edith walifunga ndoa mwaka 1990. Edith aliuguzwa kwa miezi kadhaa nchini Morocco, na umma haukutangaziwa sababu za kifo chake. Edith alikuwa binti wa Rais wa Congo, Denis Sassou Nguessou. Mwanaharakati huyo wa mapambano dhidi ya Ukimwi alikuwa mke wa pili kwa Bongo, mke wa kwanza wa Rais huyo alikuwa, Josephine Nkama.",
"Omar Bongo\nHabari za kifo cha Rais huyo wa Gabon zilikuja wiki chache baada ya mahakama nchini Ufaransa kutaka kufanyiwa uchunguzi juu ya mali ya Rais Bongo nchini Ufaranasa. Uchunguzi kama huo pia utafanyiwa mali ya rais wa Kongo Brazzaville Dennis Sassou Nguesso na rais wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang` Nguema.\nShirika la kupambana na rushwa \"Transparency International\", tawi la Ufaransa linawalaumu viongozi hao kwa kutumia fedha za umma, kununua nyumba katika nchi za nje na pia kwa kununua magari ya kifahari, madai ambayo viongozi hao wameyakanusha.\nRipoti iliyotolewa na serikali ya Gabon ilisema kuwa, ilithibitisha kuwa rais Bongo alikuwa amelazwa katika zahanati moja nchini Uhispania lakini haikutaja chochote kuhusiana na maradhi ya saratani, baada ya madai kuwa rais Bongo alikuwa akiugua saratani ya utumbo.\nPia ripoti hiyo ilisema kuwa kiongozi huyo hajafanyiwa upasuaji wowote na kuvilaumu vyombo vya habari kwa kueneza uvumi wenye lengo la kuivuruga Gabon.",
"Historia ya Ufaransa\nMakoloni yake mengi katika Afrika yalipata [[uhuru]] bila vita mnamo [[1960]]. Ila Aljeria, iliyowahi kutangazwa kuwa sehemu ya Ufaranya yenyewe, ilipata uhuru wake baada ya vita vikali vya kupigania uhuru vya miaka 1954 - [[1962]].\n[[File:Bundesarchiv B 145 Bild-F011021-0002, Köln, Staatsbesuch de Gaulle, Begrüßung Adenauer.jpg|thumb|right|De Gaulle na [[Konrad Adenauer]] wa Ujerumani mwaka [[1961]].]]\nKatika kipindi hiki cha vurugu [[jenerali]] [[Charles de Gaulle]] alichaguliwa kuwa [[rais]] chini ya katiba mpya iliyounda mfumo wa rais kama kiongozi wa [[serikali]] mwenye [[mamlaka]] makubwa.",
"Omar Bongo\nAkiwa ziarani nchini Cameroon waziri mkuu wa Ufaransa Francois Fillon alisema kuwa rais Bongo alikuwa katika hali nzuri hadi kufikia mapema hapo jana.\nMnamo tarehe sita mwezi huu rais Bongo anayeitawala Gabon kwa miaka arobaini na moja sasa, alisema kuwa angesitisha kwa muda shughuli zake ili kupumzika na pia kuomboleza kifo cha mkewe aliyeaga dunia mwezi machi mwaka huu.\nMkewe Edith Lucie Bongo ambaye ni mtoto wa rais wa kongo Brazzaville Denis Sassou Ngueso, aliaga dunia nchini morrocco akiwa na umri wa miaka arobaini na tano, baada ya kuugua kwa muda mrefu.\nHabari kutoka afisi ya rais zilisema kuwa, rais Bongo alipatwa na mshutuko baada ya kifo cha mkewe.",
"Omar Bongo\nEl Hadj Omar Bongo Ondimba (30 Desemba 1935 – 8 Juni 2009) alikuwa Rais wa nchi ya Gabon tangu mwaka wa 1967. Baadhi ya marais barani Afrika, Bongo ameshika urais kwa muda mrefu kabisa. Alimfuata Leon M'ba akiwa na umri wa miaka 31 tu, na wakati ule alikuwa rais kijana kabisa duniani. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa \"Albert-Bernard Bongo.\nKiongozi huyo mwanzoni alitambulika kama Albert Benard Bongo kabla ya baadae kusilimu na kuitwa Omari Bongo. baada ya kumaliza masomo yake ya awali na sekondari mjini Brazzaville, Bongo alianza kazi katika shirika la umma lililokuwa likishughulika na masuala ya posta na simu lakini baadae aliingia kwenye mafunzo ya kijeshi na taratibu ukawa mwanzo wa kujikita kwenye siasa.",
"Gabon\nMwaka 1990, udhaifu wa pesa CFA frank uliacha Gabon katika shida ya kulipa deni za kimataifa; Ufaransa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) wameipa Gabon mkopo na usaidizi kwa uelewano kwamba Gabon itageuza uchumi wake barabara.",
"John Garang\nSPLA ilipata msaada wa Libya, Uganda na Ethiopia. Garang na jeshi lake walidhibiti sehemu kubwa ya mikoa ya kusini mwa nchi, iliyoitwa \"Sudan Mpya\" . Yeye alidai kuwa 'ujasiri wa askari wake kutoka kwa \"uthibitisho kwamba sisi tunapambana vita vya haki. Hilo ni jambo ambalo Sudan Kaskazini na watu wake hawana. \" Wakosoaji walipendekeza motisha za fedha kwa uasi wake, wakibainisha kuwa kiasi kikubwa cha mafuta ya Sudan kiko katika kusini mwa nchi.\nGarang alikataa kushiriki katika serikali ya mpito mwaka wa 1985 au uchaguzi wa 1986, na kubaki akiwa kiongozi wa waasi. Hata hivyo, SPLA na serikali zilitia saini mkataba wa amani tarehe 9 Januari 2005 mjini Nairobi, Kenya. Tarehe 9 Julai 2005, aliapishwa kama makamu wa rais, cheo cha pili kwa ukuu katika nchi, kufuatia sherehe ambapo yeye na Rais Omar al-Bashir walitia saini katiba ya kugawana madaraka. Yeye pia alikuwa kiongozi wa utawala wa kusini mwa Sudan yenye uhuru mdogo kwa miaka sita kabla ya kufanyika kwa kura ya maoni ya uwezekano wa Kuganywa. Hakuna Mkristo au mtu kutoka kusini aliwahi kushikilia cheo cha juu kama hicho serikalini. Akizungumza baada ya sherehe, Garang alisema, \"Mimi nawapongeza watu wa Sudan, hii si amani yangu au amani ya al-Bashir, ni amani ya watu wa Sudan.\""
] | 18
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.