id stringlengths 1 6 | url stringlengths 31 202 | title stringlengths 1 120 | text stringlengths 8 182k |
|---|---|---|---|
2 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia | Akiolojia | Akiolojia (kutoka Kiyunani αρχαίος = zamani na λόγος = neno, usemi) ni somo linalohusu mabaki ya tamaduni za watu wa nyakati zilizopita. Wanaakiolojia wanatafuta vitu vilivyobaki, kwa mfano kwa kuchimba ardhi na kutafuta mabaki ya majengo, makaburi, silaha, vifaa, vyombo na mifupa ya watu.
Akiolojia na historia
Tofaut... |
10 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Daktari | Daktari | Daktari (au dokta; wingi wake unaundwa kwa kutanguliza ma-) ni neno lenye asili ya Kilatini ("doctor") lililoingia Kiswahili kwa kupitia Kiingereza. Hutumiwa kwa maana mbili:
1) Mtaalamu aliyepata mafunzo maalum kwenye chuo kikuu cha kutibu maradhi ya wagonjwa. Mtu wenye ujuzi wa kutibu anaitwa pia mganga (wa), tabibu... |
16 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia | Historia | Historia (kutoka Kigiriki ιστορια, historia; pia "tarehe" kutoka Kiarabu تاریخ tarih kwa maana ya "historia": pia tena "mapisi") ni somo kuhusu maisha ya binadamu na utamaduni wao wakati uliopita.
Mara nyingi neno hilo lina pia maana ya maarifa yoyote kuhusu wakati uliopita, yawe au yasiwe maarifa ya watu (kwa mfano "... |
17 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika | Historia ya Afrika | Historia ya Afrika ni historia ya bara hilo lililo asili ya binadamu wote.
Kwa ujumla, historia ni kumbukumbu ya maisha ya mwanadamu duniani, hasa ile tarehe iliyosajiliwa na kuhifadhiwa katika vitabu, maandishi mbalimbali, na simulizi au hekaya za mapokeo. Ingawa historia iliyobebwa katika simulizi na hekaya huchuku... |
20 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Hesabu | Hesabu | Hesabu (afadhali: Hisabati kutoka neno la Kiarabu vilevile) ni somo linalohusika na idadi na jinsi tunavyoweza kuhesabu kwa kutumia hasa kanuni zifuatazo: kujumlisha, kutoa, kuzidisha na kugawa n.k.
Hesabu ni sehemu ya msingi ya nadharia ya namba.
Hisabati |
24 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jiografia | Jiografia | Jiografia ni somo la Dunia na vipengele vyake, wakazi wake, na maajabu yake.
Neno la Kiswahili jiografia linafuata matamshi ya Kiingereza ya neno la Kigiriki "γεωγραφία", geo-grafia kutoka gê "dunia" na graphein "kuandika". Lina maana ya "kuandika kuhusu Dunia". Neno hili lilianza kutumiwa kwa mara ya kwanza na mwana... |
30 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto | Kiesperanto | Kiesperanto ni lugha ya kupangwa inayozungumzwa zaidi duniani kati ya lugha hizi. Ilipangwa na Ludwik Lejzer Zamenhof, myahudi aliyetoka mjini Białystok, nchini Urusi (siku hizi ni sehemu ya nchi ya Poland). Alitoa kitabu cha kwanza cha lugha hii mwaka 1887 baada ya kuitengeneza kwa miaka karibu kumi. Nia yake ilikuwa ... |
31 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20ya%20kuundwa | Lugha ya kuundwa | Lugha ya kuundwa (au lugha unde) ni lugha ambayo misamiati na sarufi zake zimetungwa na watu badala ya kukua kama sehemu ya utamaduni wa umma fulani. Kwa kawaida zinaundwa kwa ajili ya kuwasiliana kati ya watu sawasawa na lugha asilia. Nyingi zinatengenezwa ili kuwa lugha saidizi za kimataifa, lakini nyingine zinaundwa... |
32 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha | Lugha | Lugha (kutoka neno la Kiarabu: لغة) ni utaratibu wa kuwasiliana kati ya binadamu (wengine wanadai hata kati ya viumbe wenye akili).
Somo la lugha linaitwa maarifa ya lugha au isimu.
Mwaka wa 2008 ulikuwa Mwaka wa Lugha wa Kimataifa.
Maana ya neno "lugha"
Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zenye maana na zilizokubal... |
33 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20asilia | Lugha asilia | Lugha asilia ni lugha ambayo ilikua kama sehemu ya utamaduni wa umma fulani ambao watu wake wanaiongea kama lugha mama. Ni kinyume cha lugha ya kuundwa (lughaundwe).
Mara nyingine lugha asilia maana yake ni lugha yoyote ambayo inaweza kuzungumzwa na watu, huku lugha za kompyuta na za kuandaa programu zinaitwa lugha za... |
65 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Madola | Madola | Katika mabara, lile lenye nchi nyingi zaidi ni Afrika likiwa na nchi au madola 54, likifuatiwa na bara la Ulaya likiwa na madola 48, kisha Asia likiwa na madola 44, halafu Amerika ya Kaskazini pamoja na Amerika ya Kati likiwa na madola 23, na baada yake ni Australia na Pasifiki (Oshania) likiwa na madola 14, na mwishow... |
71 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi | Sayansi | Sayansi ni maarifa yanayopatikana kwa kufanya vitendo, kutazama na kujaribu kweli ambazo zimebainishwa hazijathibitishwa.
Mara nyingi Galileo Galilei anahesabiwa kuwa baba wa sayansi ya kisasa.
Aina za sayansi
Kuna sayansi mbalimbali ambazo huainishwa katika makundi yafuatayo:
Sayansi Asili k.m.
Biolojia
Jiogra... |
72 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria | Sheria | Sheria (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza law ) ni mfumo wa kanuni, ambazo kwa kawaida hutekelezwa kupitia seti ya taasisi maalumu. Inaunda siasa, uchumi na jamii kwa njia mbalimbali na huratibu mahusiano baina ya watu.
Sheria ya mkataba huongoza kila kitu, kuanzia kununua tiketi ya basi hadi biashara katika maso... |
73 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Siasa | Siasa | Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika ngazi mbalimbali za jamii, kama vile mji, taifa, au hata dunia nzima (siasa ya kimataifa).
Sehemu muhimu ya siasa ni majadiliano kati ya watu mbalimbali wenye nguvu au mamlaka.
Katika demokrasia kila mtu ana kiasi fulani cha nguvu, kwa hiyo siasa ya demokrasia ina maana ya wat... |
78 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ushairi | Ushairi | Ushairi ni utungo wa kisanaa ulio na madhumuni ya kutumbuiza au kuelimisha. Tena, ushairi ni tawi mojawapo la fasihi andishi. Kinyume chake ni nathari.
Inawezekana kutunga mashairi yenyewe au kutumia lugha ya kishairi katika aina nyingine za sanaa, kwa mfano tamthiliya au nyimbo.
Ushairi una historia ndefu. Kwa mfano... |
654 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20saidizi%20ya%20kimataifa | Lugha saidizi ya kimataifa | Lugha saidizi ya kimataifa ni lugha ya kuundwa iliyoundwa kwa ajili ya mawasiliano kati ya watu toka mataifa mbalimbali. Lugha saidizi ya kimataifa inayozungumzwa zaidi ni Kiesperanto. Nyingine ni kama Kivolapuki, Kiido, Kiinterlingua na Kislovianski.
Lugha saidizi ya kimataifa
nl:Kunsttaal#Internationale hulptalen |
660 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Hisabati | Hisabati | Hisabati ni somo linalohusika na idadi, upimaji na ukubwa wa vitu.
Kwa ujumla linahusika na miundo na vielezo.
Hisabati linaundwa na masomo mbalimbali, kama hesabu, jiometria na aljebra.
Neno hisabati katika lugha ya Kiswahili limetokana na neno la Kiarabu حسابات (halisi: hesabu (wingi)).
Somo hili huweza kutumik... |
692 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheng | Sheng | Sheng ni lugha ya mitaani nchini Kenya inayochanganya Kiswahili na Kiingereza pamoja na lugha mbalimbali za kienyeji kama vile Kikikuyu, Kijaluo n.k. Sanasana hutumiwa na vijana katika mji wa Nairobi. Hata hivyo lugha hii inasambaa katika sehemu mbalimbali za Kenya na watu wa matabaka mbalimbali wanaitumia. Sheng inatu... |
693 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiswahili | Kiswahili | Kiswahili ni lugha ya Kibantu yenye misamiati mingi ya Kiarabu (35%), lakini sasa ya Kiingereza pia (10%), inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki.
Lugha hii ina utajiri mkubwa wa misamiati, misemo, methali, mashairi, mafumbo, vitendawili na nyimbo. Kiswahili hutumika kufundishia shuleni na kuna vitabu... |
882 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mwanzo | Mwanzo | <center>
Takwimu ya Wikipedia ya Kiswahili
<small>
Idadi ya makala:
Idadi ya kurasa zote: (pamoja na kurasa za watumiaji, majadiliano, msaada n.k.)
Idadi ya hariri:
Idadi ya watumiaji waliojiandikisha:
Idadi ya wakabidhi:
Idadi ya watumiaji hai: (Watumiaji waliojiandikisha na kuchangia katika muda wa siku 30 ... |
888 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiarabu | Kiarabu | Kiarabu (ar.: العَرَبِيَّة, al-ʻarabiyyah, kwa kirefu al-luġatu al-ʿarabiyya) ni lugha ya Kisemiti inayotumiwa na watu milioni 206 kama lugha ya kwanza na milioni 246 wa ziada kama lugha ya pili. Ilhali kuna lahaja nyingi, Kiarabu sanifu (ar. الفصحى fuṣḥā) ni lugha rasmi ya nchi 22 za Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na ya... |
889 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Uislamu | Uislamu | Uislamu (kwa Kiarabu: الإسلام al-islam) ni dini inayotokana na mafunzo ya Mtume Muhammad.
Wafuasi wa imani hiyo huitwa "Waislamu" na wanakadiriwa kuwa milioni 1,800 hivi. Hivyo ni dini ya pili duniani yenye wafuasi wengi baada ya Ukristo wenye wafuasi milioni 2,400.
Uislamu ni ile imani kuwa muumba ni mmoja tu kwa ... |
890 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kurani | Kurani | Kurani (kwa Kiarabu: القرآن, Qur'an) ni kitabu kitukufu cha Uislamu ambacho kinaaminiwa na Waislamu kuwa ni "Neno la Allah (Mwenyezi Mungu)". Kitabu hicho kwao ni tofauti kabisa na maandiko ya dini nyingine kwa maana hicho kinaaminika kwamba kimeandikwa moja kwa moja na Mwenyezi Mungu, kupitia mtume wake wa mwisho, Muh... |
891 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Hadithi%20za%20Mtume%20Muhammad | Hadithi za Mtume Muhammad | Hadithi au Sunnah ni maneno na vitendo ambavyo Mtume Muhammad alikuwa akisema au akifanya katika kipindi chake cha utume. Hadithi hizi ni mmoja kati ya miongozo ya imani kwa Waislamu.
Hadithi hizi zinajumuisha pia mambo aliyoyaona au kuyasikia katika muda wa utume wake akalinyamazia kimya au akawa hakulipinga na akal... |
904 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ukristo | Ukristo | Ukristo (kutoka neno la Kigiriki Χριστός, Khristos, ambalo linatafsiri lile la Kiebrania מָשִׁיחַ, Māšîăḥ, linalomaanisha "Mpakwamafuta" ) ni dini inayomwamini Mungu pekee kama alivyofunuliwa kwa Waisraeli katika historia ya wokovu ya Agano la Kale na hasa Yesu Kristo katika Agano Jipya ambaye ni mwanzilishi wake kati... |
921 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiingereza | Kiingereza | Kiingereza ni lugha ya jamii ya Kigermanik cha Magharibi iliyokua nchini Uingereza kwa muda wa miaka 1,400.
Leo, zaidi ya wasemaji milioni mia nne duniani wanazumgumza Kiingereza kama lugha ya kwanza. Watu wengi zaidi wanazumgumza Kiingereza kama lugha ya pili, kwa sababu ni muhimu sana kwenye nyanja za mawasiliano, ... |
923 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika | Afrika | Afrika ni bara la pili duniani kwa ukubwa, likiwa na eneo la kilometa za mraba zipatazo 30,370,000 na kwa idadi ya wakazi, hao wakiwa 1,225,080,510 (mwaka 2016). Asia ndiyo bara kubwa pekee zaidi ya Afrika.
Jina
Neno "Afrika" limetokana na lugha ya Kilatini ya Roma ya Kale. kwa jina hilo Waroma wa Kale walitaja eneo... |
1163 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kuki | Kuki | Kuki ni tafsiri ya muda ya neno la Kiingereza cookie, ambalo maana yake asili ni biskuti au keki ndogo, lakini katika utarakilishi linatumika ili kompyuta yenye kurasa za tovuti iweze kuwasaliana na watazamaji.
Programu za tovuti hizi zinahifadhi habari kadhaa za mtazamaji au mtumiaji (k.m. jina la mtumiaji, neno la s... |
1165 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Panzi | Panzi | Panzi ni aina za wadudu wanaokula mimea. Wameainishwa katika nusuoda Caelifera ya oda Orthoptera. Takriban spishi zote huchupa mbali kwa kutumia miguu yao ya nyuma ambayo ina nguvu sana. Nyingi zinaweza kuruka angani. Panzi wana vipapasio vifupi kuliko mwili wao. Panzi wakubwa ambao wanajikusanya kwenye makundi makubwa... |
1166 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Nzige | Nzige | Nzige ni jamii ya panzi wenye uwezo wa kujikusanya kwenye makundi makubwa na kuruka umbali mrefu kwa pamoja. Wanao huitwa tunutu. Nzige wanapokuwa wametawanyika mmojammoja huishi kama panzi wa kawaida. Wanapozaliana na kuongezeka idadi hujikusanya katika makundi. Makundi ya tunutu husafiri kuelekea upande mmoja na kula... |
1169 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Muhammad | Muhammad | Muhammad (kwa Kiarabu "Mwenye kusifika sana"; jina kamili kwa kirefu ni محمد بن عبد الله بن عبد ﺍﻟﻤﻄﻠﺐ ﺍﻟﻬﺎﺷﻤﻲ Muhammad bin 'Abd Allāh bin 'Abd al-Muţţalib al-Hāshimī) anaaminika katika dini ya Uislamu kuwa ni mtume wa mwisho wa Mungu (Allah) kwa binadamu.
Utoto wake
Muhammad alizaliwa yatima kwani baba yake alifari... |
1171 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Fizikia | Fizikia | Fizikia (kutoka neno la Kigiriki φυσικός, physikos, "ya kimaumbile", ambalo tena linatokana na φύσις, physis, "umbile") ni fani ya sayansi inayohusu maumbile ya ulimwengu, hususan asili ya dunia na viumbe vyote.
Ni taaluma yenye kushughulika na maada na uhusiano wake na nishati.
Fizikia imetoa mchango mkubwa katika s... |
1174 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mwenyezi%20Mungu | Mwenyezi Mungu | Mwenyezi Mungu katika lugha ya Kiswahili ni jina linalotumika kwa Muumba wa kila kitu, Mwenye kuabudiwa kwa haki, kinyume na neno mungu ambalo linamaanisha chochote au yeyote anayeabudiwa ikiwa kwa haki au si kwa haki.
Neno Mwenyezi linaunganisha Mwenye na enzi na kumpatia Mungu sifa ya kuweza yote, bila kuzuiliwa na... |
1175 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Dunia | Dunia | Dunia (; kutoka neno la Kiarabu دنيا, dunyaa; wakati mwingine pia: ardhi na kwa neno asili la Kibantu: nchi) ni gimba la angani ambapo juu yake tunaishi sisi binadamu na viumbehai wengine wengi, tukipata mahitaji yetu, kuanzia hewa ya kutufaa na maji.
Dunia ni mojawapo ya sayari nane zinazozunguka Jua letu katika ang... |
1178 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Asia | Asia | Asia ni bara kubwa kabisa kuliko mabara yote mengine ya dunia. Bara hili lina eneo la kilomita za mraba 44,579,000 (maili za mraba 17,212,000), ambalo ni sawa na asilimia 30% ya ardhi yote. Wakazi wa bara la Asia ni 3,701,000,000 kwa mujibu wa makisio 2003.
Bara la Asia lina nchi 44 na visiwa mbali mbali vya madola mb... |
1182 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Isa | Isa | Isa ni umbo la jina Yesu katika Qurani na pia katika lugha mbalimbali zilizoathiriwa na Uislamu. Ukurasa huu unahusu imani ya Uislamu kumhusu Yesu kadiri ya Kurani.
Kitabu hicho kilichoandikwa miaka 600 hivi baada ya Kristo kina aya 93 zinazomhusu, lakini hakileti mfululizo wa habari za maisha yake wala za mafundisho... |
1183 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bara | Bara | Bara (au kontinenti) ni pande kubwa la nchi kavu la Dunia linalozungukwa na bahari. Kwa kawaida tunatofautisha mabara 7 ya Afrika, Amerika Kaskazini, Amerika Kusini, Antaktiki, Asia, Australia, na Ulaya.
Wazo la bara
Neno "bara" lamaanisha pande kubwa la nchi kavu , tofauti na bahari au visiwa vidogo karibu na pwani y... |
1191 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Tanzania | Tanzania | Tanzania (jina rasmi: Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi iliyoko Afrika ya Mashariki ndani ya ukanda wa maziwa makuu ya Afrika. Imepakana na Uganda na Kenya upande wa kaskazini, Bahari Hindi upande wa mashariki, Msumbiji, Malawi na Zambia upande wa kusini, Kongo, Burundi na Rwanda upande wa magharibi.
Eneo lina k... |
1201 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Uhindi | Uhindi | Uhindi (pia: India) ni nchi kubwa ya bara la Asia, upande wa kusini, ikienea hasa katika rasi kubwa ya Bahari ya Hindi.
Kwa eneo ina nafasi ya saba duniani, lakini kwa idadi ya wakazi (1,352,642,280 mwaka 2018) ni nchi ya pili baada ya China. Kati ya nchi za kidemokrasia ndiyo yenye watu wengi zaidi duniani. Tena ina... |
1203 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki | Afrika ya Mashariki | Afrika ya Mashariki ni sehemu ya bara la Afrika ambayo iko upande wa mashariki, ikipakana na Bahari ya Kihindi.
Kadiri ya Umoja wa Mataifa Afrika ya Mashariki ina nchi 18 zifuatazo:
(mji mkuu Bujumbura)
(mji mkuu Jibuti (mji))
(mji mkuu Asmara)
(mji mkuu Addis Abeba)
(mji mkuu Nairobi)
Komori (mji mkuu M... |
1204 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Simu | Simu | Simu (kutoka Kiarabu سیم, sim, inayomaanisha "waya") ni chombo cha mawasilianoanga kinachotumia umeme.
Matumizi ya simu ni kwa ajili ya watu wawili walio katika sehemu mbili tofauti kuongea.
Awali simu ilihitaji iunganishwe na nyaya, lakini leo hii inaweza kutumia redio. Hiyo inaitwa nyayatupu, siwaya au simu bila ... |
1208 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiido | Kiido | Kiido ni lugha ya kupangwa. Inafanana sana na Kiesperanto, lakini haizungumzwi na watu wengi kama Kiesperanto.
Serufi
Nomino (majina) zote zinahitimu kwa kiambishi tawali -o, kwa mfano "arbo" (mti). Wingi wa nomino unahitimu kwa -i (arbi = miti).
Vivumishi vinahitimu kwa kiambishi tawali -a, kwa mfano "alta" (-refu... |
1663 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mungu | Mungu | Mungu ni jina lenye asili ya Kibantu linalotumika kwa yeyote anayesadikiwa katika dini mbalimbali kuwa na uhai wa hali ya juu.
Kati ya wafuasi wa dini hizo, wengi wanaona kuwa Umungu, kwa jinsi ulivyo au unavyofirika, haukubali mgawanyiko. Hasa katika Uyahudi, Ukristo na Uislamu wanasisitiza umoja wa Mungu kuwa ndio m... |
1664 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Volkeno | Volkeno | Volkeno (pia: volkano au volikano) ni mahali ambako zaha inatoka nje ya uso wa ardhi. Mara nyingi - lakini si kila mahali - volkeno imekuwa mlima. Volkeno huwa na kasoko yaani shimo ambako zaha na gesi zinatoka nje.
Asili ya jina
Asili ya jina ni mungu wa dini ya Roma ya Kale aliyeitwa "Vulcanus". Kati ya miungu ya Ki... |
1665 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Tofaa | Tofaa | Tofaa (pia: tufaha; kutoka kar. تفاح tofah; kwa Kiingereza: apple) ni tunda la mtofaa. Ni kati ya matunda yanayovunwa sana duniani. Maua nyeupe hutoa tunda lenye umbo mviringo na kipenyo cha sentimita 5 - 9.
Asili ya mimea iko Asia. Leo kuna takriban aina 7,500 za matofaa. Mavuno ya kila mwaka hufikia tani milioni 55.... |
1667 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiazi%20cha%20kizungu | Kiazi cha kizungu | Kiazi cha kizungu, kiazi ulaya, kiazi mviringo au mbatata ni mmea wa chakula uliomo katika familia ya Solanaceae. Chakula ni sehemu nene za mizizi yake (kiazi) yenye wanga, vitamini na madini. Sehemu bichi zinazoonekana juu ya ardhi haziliwi ni sumu.
Viazi hivi ni chakula muhimu kimataifa ni chakula kikuu katika nying... |
1675 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Seattle%2C%20Washington | Seattle, Washington | Seattle ni mji wa jimbo la Washington (ncha ya kaskazini magharibi ya Marekani). Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2018, mji una wakazi wapatao milioni 3.87 wanaoishi katika mji huu.
Mji uko mita 0-158 juu ya usawa wa bahari.
Seattle ni njia kuu ya biashara kati ya Marekani na Asia, ukiwa na bandari y... |
1676 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kenya | Kenya | Jamhuri ya Kenya ni nchi iliyoko Afrika Mashariki katika ikweta, kando ya Bahari ya Hindi.
Kenya imepakana na Ethiopia (kaskazini), Somalia (kaskazini mashariki), Tanzania (kusini), Uganda na Ziwa Victoria (magharibi), kisha Sudan Kusini (kaskazini magharibi).
Kenya ni nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Masha... |
1677 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mombasa | Mombasa | Mombasa ni mji mkubwa wa pili wa Kenya na wenye bandari muhimu zaidi Afrika Mashariki. Mji huu uko kwenye mwambao wa Bahari Hindi.
Baada ya kuundwa kwa serikali ya ugatuzi, Mombasa umekuwa mji mkuu wa kaunti ya Mombasa.
Mombasa ni kitovu cha utalii wa pwani ya Kenya. Watalii wengi hufika kupitia Uwanja wa Ndege wa ... |
1679 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Togo | Togo | Togo ni nchi ya Afrika ya Magharibi inayofikia kwenye mwambao wa Ghuba ya Guinea (bahari ya Atlantiki) ikipakana na Benin upande wa mashariki, Burkina Faso kaskazini na Ghana mashariki.
Idadi ya wakazi ilikuwa zaidi ya milioni 8 u nusu mwaka 2022.
Mji mkuu ni Lome.
Jiografia
Togo ni nchi ndogo katika Afrika yenye k... |
1686 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Pangani | Pangani | Pangani ni jina la mto, wilaya na mji katika Tanzania.
* Mto wa Pangani unabeba maji ya Milima ya Meru, Kilimanjaro, Pare na Usambara kwenda Bahari Hindi. Mdomo wake uko mjini Pangani.
* Wilaya ya Pangani ni kati ya wilaya za mkoa wa Tanga.
* Mji wa Pangani ni makao makuu wa wilaya ya Pangani iliyomo mkoa wa Tanga u... |
1696 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mhanga | Mhanga | Mhanga (pia muhanga, fundi-mchanga, kiharara, kukukifuku au loma; jina la kisayansi: Orycteropus afer) ni mnyama wa Afrika aliye spishi pekee ya oda Tubulidentata ambayo inaishi hadi sasa.
Wanatokea pande nyingi za Afrika kusini kwa Sahara. Wahanga hula sisimizi na mchwa.
Mhanga
Wanyama wa Afrika
Wanyamapori |
1701 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Wamasai | Wamasai | Wamasai ni kabila la watu wanaopatikana Kenya na Tanzania. Kwa sababu ya mila zao, mavazi tofauti na kuishi karibu na mbuga nyingi za Afrika Mashariki, ni miongoni mwa makabila yanayojulikana zaidi hata nje ya Afrika.
Wao wanazungumza Maa, mojawapo ya lugha za familia ya lugha za Kinilo-Sahara inayohusiana na Kidin... |
1705 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ulaya | Ulaya | Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun; inaitwa pia Uropa) ni bara lenye eneo la km² 10,600,000 tu, lakini wakazi ni milioni 747 .
Wengi wenye asili ya Ulaya wakati wa ukoloni walitawanyika duniani, hasa Amerika, wakiathiri kote upande wa lugha, utamaduni na dini.
Utawala
Katika karne ya 20, baad... |
1706 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Lituanya | Lituanya | Lituanya (au Lituania) ni nchi huru iliyoko Kaskazini Mashariki mwa Ulaya. Inajulikana rasmi kama Jamhuri ya Lituania.
Inapakana na Latvia, Belarus, Polandi na Russia.
Ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya.
Mji mkuu wa Lituania ni Vilnius.
Jiografia
Lituanya iko kwenye mwambao wa Bahari ya Baltiki.
Miji mikubwa
Kau... |
1707 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Europa | Europa | Europa ni neno katika lugha mbalimbali lenye asili ya Kigiriki "Ευρώπη" la kutaja
bara la Ulaya
Europa (mitholojia), binti wa mfalme katika masimulizi ya dini ya Wagiriki wa Kale aliyekuwa mpenzi wa mungu mkuu Zeus
Europa (mwezi), mwezi wa pili kati ya miezi ya Mshtarii
52 Europa, asteroidi katika mfumo wa jua
... |
1749 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Dodoma | Dodoma | Dodoma ni jina la
Mji wa Dodoma ambao ni Mji Mkuu wa Tanzania
Mkoa wa Dodoma
na Wilaya ya Dodoma (mjini na kijijini).
Pia ni makao makuu ya chama tawala Tanzania, Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Tanzania
Makala zinazotofautisha maana |
1750 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Shilingi | Shilingi | Shilingi ni pesa inayotumika kwa malipo halali katika nchi za Tanzania, Kenya, Uganda na Somalia.
Historia ya Shilingi
Asili ya jina ni kitengo cha kihistoria cha pesa katika nchi mbalimbali za Ulaya kama vile Austria, Uswisi, Uingereza, Poland, Denmaki, Norwei na Uswidi.
Katika nchi nyingi kati ya hizo pesa hiyo ha... |
1751 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilimanjaro%20%28Volkeno%29 | Kilimanjaro (Volkeno) | Kilimanjaro ni jina la mlima mrefu kuliko yote barani Afrika. Mlima huo uko nchini Tanzania katika Mkoa wa Kilimanjaro. Una urefu wa mita 5,895 (futi 19,340).
Hali halisi Kilimanjaro ni zaidi ya mlima tu, ni kama safu ndogo ya milima mitatu: Kibo, Mawenzi na Shira. Hiyo mitatu inaonekana kama vilele vitatu vya mlima m... |
1752 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Nyerere | Julius Nyerere | Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Butiama, Mkoa wa Mara, pembezoni mwa Ziwa Nyanza, 13 Aprili 1922 - London, Uingereza, 14 Oktoba 1999) alikuwa rais wa kwanza wa Tanzania, na mara nyingi anatajwa kama "Baba wa Taifa" kwa jinsi alivyoathiri nchi hiyo.
Ndiye mwasisi wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea iliyotangazwa has... |
1753 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mbege | Mbege | Mbege ni kileo asili cha Wachagga, wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro.
Mbege hutengenezwa kwa ndizi mbivu, kimea cha ulezi, na maji.
Mara nyingi mbege hutengenezwa na wanawake na hutumika katika sherehe na matukio mbalimbali kama vile harusi, misiba, kipaimara, kuzaliwa kwa mtoto, n.k. Mbege hutumiwa pia kama faini kwe... |
1756 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilimanjaro | Kilimanjaro | Kilimanjaro ni jina la Kiswahili linalomaanisha :
Mlima wa Kilimanjaro katika Tanzania ambao ni mlima kubwa kabisa katika bara la Afrika
Hifadhi ya Kilimanjaro inayozunguka kilele cha mlima
Mkoa wa Kilimanjaro ni mkoa wa Tanzania katika sehemu ya Mlima wa Kilimanjaro
Kilimanjaro (Moshi Mjini), kata ya Moshi Mjini
... |
1757 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Nchi%20za%20Maziwa%20Makuu | Nchi za Maziwa Makuu | Nchi za Maziwa Makuu ni nchi zinazopakana na maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki ambazo ni Tanzania, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya na Uganda.
Kati ya maziwa makubwa yaliyoko katika eneo hili kuna
Ziwa Nyanza (Viktoria)
Ziwa Tanganyika
Ziwa Nyasa (Malawi)
Ziwa Mwitanzige (Albert]]
Ziwa Ru... |
1758 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Fasihi | Fasihi | Fasihi (kutoka neno la Kiarabu فصاحة, fasaha kwa maana ya ulimbi au "literacy" kwa Kiingereza) ni utanzu (tawi) wa sanaa ambao hutumia lugha ya mazungumzo au maandishi ili kufikisha (kuwasilisha) ujumbe kwa hadhira husika. Ni ufundi wa kuwasilisha mawazo au ujumbe ulio katika fikra za binadamu.Fasihi ni sanaa inayotumi... |
1759 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Intaneti | Intaneti | Intaneti (kutoka Kiingereza Internet) ni mfumo wa kushirikiana kwa tarakilishi nyingi unaowezesha watu mbalimbali duniani kuwasiliana baina yao. Kupitia mtandao huo, watu huweza kutembelea tovuti mbalimbali, kupiga gumzo, na kuandikiana barua pepe.
Intaneti ni mfumo wa kimataifa wa mitandao ya tarakilishi inayotumia i... |
1760 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Blogu | Blogu | Blogu ni teknolojia mpya inayowezesha watu binafsi kuchapa maoni na fikra zao katika mtandao wa tarakilishi maarufu kama wavuti au intaneti. Blogu inaweza kuchukuliwa kama ni shajara pepe.
Neno la Kiswahili "blogu" linatokana na neno la Kiingereza, "blog", ambalo limetokana na neno lingine, "weblog".
Kimsingi, blogu... |
1773 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jua | Jua | Jua (alama: ) ni kitovu cha mfumo wa Jua wenye sayari nane, sayari vibete na magimba mengi madogo. Dunia ni sayari ya tatu katika mfumo huu. Jua ni nyota iliyo karibu na Dunia yetu kuliko nyota nyingine zote.
Umbo la Jua
Umbo la Jua linakaribia kuwa tufe kamili. Maada yake ni utegili yaani gesi ya joto sana inayoshika... |
1774 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Wachagga | Wachagga | Wachagga ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu (lakini pia mchanganyiko wa damu, hasa ya Kikushi) wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaro, mkoani Kilimanjaro.
Wachagga ni kabila la tatu kwa ukubwa nchini Tanzania. Takwimu za mwaka 2003 zinaonyesha kuwa idadi yao ni watu 2,000,000.
Shughuli ku... |
1775 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Djibril%20Diallo | Djibril Diallo | Dakta Djibril Diallo ni mzaliwa wa Senegal. Amewahi kuwa mkurugenzi wa mawasiliano wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda la Umoja wa Mataifa, mshauri maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na mkutano wa kimataifa wa haki za binadamu. Tena alikuwa waziri nchini Mali.
Hivi sasa anahudumia ofisi ya Umoja ya Ma... |
1776 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Abedi%20Amani%20Karume | Abedi Amani Karume | Sheikh Abeid Amani Karume alikuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar. Alizaliwa mwaka 1905 na kufariki tarehe 7 Aprili 1972 kwa kupigwa risasi.
Karume aliongoza nchi baada ya mapinduzi yaliyomwangusha Sultani aliyekuwa akitawala Zanzibar hadi mwanzoni mwa mwaka 1964.
Baada ya miezi mitatu Zanzibar iliungana na Tanganyika i... |
1777 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Orodha%20ya%20vyama%20vya%20siasa%20Tanzania | Orodha ya vyama vya siasa Tanzania | Mfumo wa vyama vingi ni hali ya kuwa na chama zaidi ya kimoja,katika nchi moja.Madhumuni ya kuwa na vyama vingi vya siasa ni kuleta ushindani wa kisiasa,ili kuleta maendeleo ya nchi,upinzani wa kisiasa sio uadui kama watu wengi kwenye nchi zinazoendelea wanavyodhani,kuwa na vyama vingi ni kuongeza wigo wa demokrasia ka... |
1778 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Nelson%20Mandela | Nelson Mandela | Nelson Rolihlahla Mandela (18 Julai 1918 - 5 Desemba 2013) alikuwa mwanasiasa nchini Afrika Kusini, kiongozi wa mapambano dhidi ya siasa ya ubaguzi wa rangi (Apartheid), mfungwa jela kwa miaka 27 halafu rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia katika nchi yake.
Alikuwa mwanasheria na mwanachama, baadaye kiongozi w... |
1781 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Rosa%20Parks | Rosa Parks | Rosa Louise McCauley Parks (4 Februari 1913 – 24 Oktoba 2005) anakumbukwa kwa uamuzi wake wa kukataa kumpisha kiti Mmarekani Mweupe kama alivyodaiwa na dereva wa basi. Uamuzi wake huo hapo mwaka 1955 ulipelekea mzozo uliosababisha Mgomo wa Mabasi wa Montgomery na kuchangia katika Vuguvugu la Haki za Kiraia Marekani. Ba... |
1782 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwame%20Nkrumah | Kwame Nkrumah | Kwame Nkrumah (21 Septemba 1909 - 27 Aprili 1972) alikuwa Rais wa kwanza wa Ghana na mmoja wa viongozi wenye nia ya kujenga Muungano wa Afrika, tena mchochezi wa falsafa ya Umajinuni.
Maisha
Miaka ya kwanza katika Ghana
Kwame Nkrumah alizaliwa mnamo mwaka 1909 katika kijiji cha Nkroful kwenye koloni la Gold Coast (le... |
1783 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ghana | Ghana | Jamhuri ya Ghana ni nchi ya Afrika Magharibi inayopakana na Côte d'Ivoire (Ivory Coast) upande wa magharibi, Burkina Faso upande wa kaskazini, Togo upande wa mashariki, na Ghuba ya Guinea upande wa kusini.
Kabla ya ukoloni Ghana ilikaliwa na idadi ya watu wa kale, hasa wa Falme za Akan, wakiwemo Waakwamu upande wa m... |
1788 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Carola%20Kinasha | Carola Kinasha | Carola Daniel Amri Kinasha (alizaliwa Longido, Mkoa wa Arusha, Tanzania, mnamo Machi mwaka 1962) ni mwanamuziki wa kike wa kitanzania.
Baada ya kumaliza masomo ya elimu ya msingi huko Longido, alihamia jijini Dar Es Salaam ambako alipata elimu ya sekondari na ya chuo kikuu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Carola... |
1789 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Wikipedia | Wikipedia | Wikipedia ni kamusi elezo huru ya lugha nyingi katika mtandao wa wavuti. Inalenga kukusanya elimu nyingi iwezekanavyo na kuisambaza kwa njia ya intaneti.
Inatumia taratibu za wikiwiki. Ni bure kabisa, na inaweza kusomwa, kuandikwa, na kuhaririwa na mtu yeyote, popote pale. Yaani kila mtu anaweza kuchangia makala akiwa... |
1790 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Dar%20es%20Salaam | Dar es Salaam | Kwa maana nyingine, tazama Mkoa wa Dar es Salaam
Dar es Salaam ni jiji kubwa kuliko yote nchini Tanzania. Pia ni jina la mkoa wake. Dar es Salaam ni mji mkongwe na wenye watu wengi zaidi katika Jumuia ya Afrika Mashariki. Katika Tanzania ndio mji wenye vitega uchumi vingi na ndio mji unaoangaliwa na watu wengi.
... |
1791 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Hindi | Bahari ya Hindi | Bahari ya Hindi ni bahari ya tatu kwa ukubwa duniani ikiwa imechukua asilimia 20 ya uso wa dunia na kuzungukwa na mabara manne.
Upande wa kaskazini imepakana na Asia ya Kusini; magharibi imepakana na Ghuba ya Uajemi, Bahari ya Shamu na Afrika; mashariki imepakana na Ghuba ya Malay, visiwa vya Sunda (Indonesia), na Au... |
1792 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Nairobi | Nairobi | Nairobi ni mji mkuu wa jamhuri ya Kenya na vilevile mojawapo ya kaunti za Kenya.
Kulingana na sensa ya mwaka 2019, Nairobi ina wakaaji 4,397,073 katika eneo la km2 696 (sq mi 269).
Pamoja na vitongoji vyake, Nairobi ni mji wa 12 kwa ukubwa barani Afrika.
Jina Nairobi limetokana na neno la Kimaasai, Enkarenairobi, ... |
1797 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bara%20la%20Antaktiki | Bara la Antaktiki | Antaktiki ni bara lililopo kwenye ncha ya kusini ya dunia, kati ya bahari za Pasifiki, Atlantiki na Bahari Hindi.
Jina "Antaktiki" linatokana na lugha ya Kigiriki likimaanisha "kinyume cha Aktiki", ambapo Aktiki ni eneo karibu na ncha ya kaskazini.
Bara hili lina eneo la kilomita za mraba milioni 14 na eneo hili lime... |
1798 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ubaguzi%20wa%20rangi | Ubaguzi wa rangi | Ubaguzi wa rangi ni kitendo cha kuthamini au kutenga binadamu kwa misingi ya rangi za ngozi. Ubaguzi wa rangi ulikuwa maarufu sana katika nchi kama Afrika Kusini kwa jina la "apartheid" na Marekani kwa jina la "segregation" ambapo huko Waafrika walikandamizwa kutokana na rangi yao katika kupata huduma mbalimbali za kij... |
1799 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Utumwa | Utumwa | Utumwa ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kummiliki binadamu mwenzake kama mali yake. Binadamu anayemilikiwa anakuwa na hadhi sawa na chombo au kifaa chochote kinachoweza kuuzwa.
Mfumo huu ulianza kabla ya uandishi kubuniwa, ukawa maarufu hasa kabla ya harakati za ukoloni duniani, mathalani kuanzia karne ya 15, ambap... |
1800 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ukoloni | Ukoloni | Ukoloni ni mfumo wa taifa moja kuvuka mipaka yake na kutawala maeneo ya mbali yanayokaliwa na watu wengine kwa nyanja za uchumi, utamaduni na jamii. Maeneo hayo yanaweza kuitwa makoloni ya kawaida au maeneo lindwa tu.
Jina
Neno "koloni" linatokana na Kilatini colonia (kupitia Kiingereza colony). Ni kwamba Roma ya Kale... |
1841 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Burundi | Burundi | {| border="1" cellpadding="2" cellspacing="0" align="right" width="330px" style="margin-left:15px; border-collapse:collapse; border-color:#f2f2f4"
|+<font size="+1">Republika y'u Burundi (Kirundi)
République du Burundi (Kifaransa)Jamhuri ya Burundi</font>
| align="center" colspan="2" |
|----
| Lugha rasmi || Kifaran... |
1843 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Eritrea | Eritrea | Eritrea ni nchi ya Afrika ya Mashariki. Mashariki na Kusini-Mashariki Eritrea ina pwani ndefu katika Bahari ya Shamu.
Upande wa Magharibi imepakana na Sudan, upande wa Kusini imepakana na Ethiopia, na Kusini-Mashariki kuna nchi ya Djibouti. Eneo hili lote hujulikana pia kama Pembe ya Afrika.
Jina
Jina la nchi limetu... |
1848 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Umoja%20wa%20Mataifa | Umoja wa Mataifa | Umoja wa Mataifa (UM) (Kiingereza: United Nations, UN) ni shirika la kiserikali ambalo malengo yake ni kudumisha amani na usalama wa kimataifa, kuendeleza uhusiano wa kirafiki kati ya mataifa, kufikia ushirikiano wa kimataifa, na kuwa kituo cha kuoanisha matendo ya mataifa. Ni umoja wa nchi zote duniani isipokuwa zile ... |
1855 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Marijani%20Rajab | Marijani Rajab | Marijani Rajabu (3 Machi 1955 - 23 Machi 1995) alikuwa mwanamuziki maarufu katika miondoko ya muziki wa dansi kutoka nchini Tanzania.
Historia yake na muziki
Historia ya gwiji huyu ilianzia siku alipozaliw,a tarehe 23 Machi mwaka 1955, katika eneo la Kariakoo. Mama yake alikuwa mama wa nyumbani wakati baba yake aliku... |
1856 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Uchoraji | Uchoraji | Kuhusu nyota angalia hapa Mchoraji (kundinyota)
Uchoraji ni sanaa ya kuweka alama au picha kwa kutumia vifaa mbalimbali vya kuchorea, kama vile kalamu ya wino au ya risasi, burashi, penseli za rangi ya nta, crayoni, makaa, choko, pastels, aina mbalimbali za erasers, markers, styluses, metali mbalimbali (kama silverpoi... |
1857 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kamusi%20elezo | Kamusi elezo | Kamusi elezo (pia: ensaiklopidia kutoka Kiingereza: encyclopedia) ni kitabu kinachokusudiwa kukusanya ujuzi wa binadamu kadiri iwezekanavyo kulingana na wingi wa kurasa zake.
Siku hizi, Wikipedia ni kamusi elezo kubwa zaidi duniani lakini si kitabu cha karatasi, ni mkusanyo wa habari kwa umbo dijitali katika intaneti... |
1858 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ngoma | Ngoma | Neno ngoma lina maana mbalimbali:
Ala ya muziki inayotumika sana barani Afrika.
Muziki unaochezwa kwa kupiga ala hiyo.
Muziki wa aina yoyote.
Kucheza na muziki wa ngoma au wa aina yoyote.
Katika lugha ya mitaani, ngoma inaweza kumaanisha virusi vya UKIMWI au Ukimwi wenyewe. Neno hili limetokana na methali ya Kiswahili... |
1859 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ellen%20Johnson-Sirleaf | Ellen Johnson-Sirleaf | Ellen Johnson-Sirleaf (alizaliwa 29 Oktoba 1938 nchini Liberia) amekuwa rais wa kwanza mwanamke barani Afrika baada ya kushinda katika uchaguzi wa mwaka 2005. Johnson-Sirleaf ameshika nyadhifa mbalimbali serikalini na katika mashirika ya kimataifa. Baada ya kumaliza masomo katika chuo kikuu cha Harvard, alifanya kazi k... |
1860 | https://sw.wikipedia.org/wiki/George%20Weah | George Weah | George Weah (alizaliwa Monrovia, 1 Oktoba 1966) ni rais wa Liberia kuanzia mwaka 2017. Kabla ya kuwa mwanasiasa aliwahi kuwa mwanakandanda mashuhuri duniani.
Maisha
Utoto, familia na kabila
Weah ni wa kabila la Kru ambalo linatoka upande wa kusini-mashariki mwa Liberia kwenye Kaunti ya Grand Kru, ambayo ni moja ya ma... |
1861 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Monrovia | Monrovia | Monrovia ni mji mkuu wa Liberia. Eneo uliko mji huu mwanzoni liliitwa Cape Mesurado na Wareno katika miaka ya 1560. Eneo hili lilianzwa kujenga mji mwaka 1822 na chama cha
American Colonization Society ikiwa ni makazi ya watu waliokombolewa toka utumwani nchini Marekani. Jina Monrovia lilitokana na jina la Rais wa Ma... |
1864 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ngoma%20%28muziki%29 | Ngoma (muziki) | Ngoma inaweza kumaanisha muziki unaochezwa na ala ya muziki inayoitwa ngoma pia.
Ngoma ni muziki na lugha ya pekee inayotumika kwa kuelezea utamaduni na historia ya nchi fulani, tunatumia lugha ya ngoma katika kuelezea hali mbalimbali za maisha yetu, kama vile huzuni, furaha, mapenzi, faraja, vitisho, shukurani na us... |
1869 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bombwe%20%28sanaa%29 | Bombwe (sanaa) | Bombwe ni sanaa ya urembo wa kuchora mwilini, kama kuchora kwa hina na kuchora kwa piko, sanaa hii hutumika zaidi na wanawake.
Tanbihi
Sanaa
Utamaduni |
1870 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Togwa | Togwa | Togwa ni kinywaji baridi kinachotengenezwa kwa nafaka au maji ya matunda. Namna ya kutengeneza ni sawa na pombe ya kawaida ila tu haikubadilika bado kuwa na alikoholi.
Togwa ndiyo itakuwa pombe ikikaa. Kwa mfano, togwa ya ulanzi ni utomvu kutoka mianzi baada ya masaa kadhaa, na ulanzi wenye pombe ni utomvu uleule kuto... |
1871 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Liberia | Liberia | Liberia (yaani Nchi ya watu huru kwa Kilatini) ni nchi iliyoko Afrika ya Magharibi. Imepakana na nchi za Ivory Coast, Guinea, na Sierra Leone.
Ni mojawapo ya nchi za Afrika ambazo hazikutawaliwa na Wazungu. Hata hivyo watu wa Liberia huongea Kiingereza sana.
Historia
Liberia ni nchi iliyoundwa na makabila 16 ya asil... |
1873 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ruth%20Perry | Ruth Perry | Ruth Fahnbulleh Perry (16 Julai 1939 - 8 Januari 2017) alikuwa kiongozi wa Liberia toka 3 Septemba 1996 hadi 2 Agosti 1997. Aliongoza nchi hiyo kama mwenyekiti wa Baraza la Taifa ambalo liliongoza nchi hiyo kufuatia kuangushwa kwa Sajenti Samuel Doe na mwisho wa urais wa Amos Sawyer. Perry alikuwa mwanachama wa chama c... |
1875 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mwai%20Kibaki | Mwai Kibaki | Mwai Kibaki (1931-2022) alikuwa rais wa tatu wa Jamhuri ya Kenya kuanzia mwaka 2002 hadi 2013 akiwa ametanguliwa na Rais wa Kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta na rais wa pili Daniel Arap Moi. Jina lake la kubatizwa ni Emilio Stanley .
Maisha
Kibaki alisoma uchumi, historia na sayansi ya siasa katika chuo kikuu cha Ma... |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.