id stringlengths 1 6 | url stringlengths 31 202 | title stringlengths 1 120 | text stringlengths 8 182k |
|---|---|---|---|
1876 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kura%20ya%20maoni | Kura ya maoni | Kura ya maoni zinatumika katika demokrasia ili kuchagua viongozi wa nchi au kuamua kama sheria fulani itumike. Kawaida kura ya maoni hupigwa na wale wote wenye umri halali wa kupiga kura ili kukubali au kukataa pendekezo, sera, sheria, mabadiliko ya katiba, katiba mpya, kukataa au kumuunga mkono kiongozi fulani. Kura y... |
1877 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kura%20juu%20ya%20katiba%20mpya%20ya%20Kenya%20%282005%29 | Kura juu ya katiba mpya ya Kenya (2005) | Kura ya maoni juu ya katiba mpya ya Kenya ilipigwa tarehe 21 Novemba 2005. Asilimia 58 ya Wakenya waliopiga kura waliikataa.
Rais wa Kenya na baadhi ya mawaziri walipiga kampeni kutaka Wakenya waiunge mkono katiba hiyo. Kundi lililokuwa likiiunga mkono katiba mpya lilikuwa likiwakilishwa na alama ya ndizi na kundi li... |
1878 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Demokrasia%20ya%20moja%20kwa%20moja | Demokrasia ya moja kwa moja | Demokrasia ya moja kwa moja ni aina ya demokrasia ambayo wananchi wote wanaweza kushiriki katika kuamua masuala ya kisiasa, kijamii, kisheria, na kiuchumi bila kutumia chombo cha uwakilishi kama vile bunge.
Uwezo huu wa wananchi kutoa maamuzi unaweza kuwapa wananchi hata uwezo wa kimahakama ingawa mara nyingi wananch... |
1879 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bunge | Bunge | Bunge ni chombo cha kutunga sheria na pia ni mmoja wa mihimili mitatu inayounda mfumo wa utawala kulingana na mgawanyo wa madaraka katika dola. Mihimili mingine ni mahakama na serikali.
Bunge ni chombo kinachotokana na mfumo wa utawala wa Westminster, ambao umerithiwa na nchi nyingi duniani kutoka Uingereza. Kutokana... |
1890 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mahakama | Mahakama | Mahakama ni mfumo wa wataalamu na kamati maalumu ambao unatafsiri na kutumia sheria katika jina la wananchi, la jamhuri au la mfalme.
Mahakama pia inatoa mfumo wa kutatua migogoro. Chini ya mfumo wa mgawanyo wa madaraka mahakama kwa ujumla haitungi wala haiundi sheria (ambayo ni kazi ya bunge) wala kutekeleza sheria ... |
1891 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Katiba | Katiba | Katiba ni sheria au kanuni zinazoaInisha jinsi ambavyo nchi, chama, au shirika vitakavyoendesha shuguli zao.
Kwa upande wa nchi, katiba ni sheria mama inayoainisha misingi mikuu ya kisiasa na kuonyesha madaraka na majukumu ya serikali. Katiba za nchi pia huainisha haki za msingi za wananchi.
Kuna aina kuu mbili za K... |
1899 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ukimwi | Ukimwi | Upungufu wa Kinga Mwilini (kwa kifupi UKIMWI; kifupisho cha Kiingereza AIDS) ni ugonjwa unaotokana na virusi ambavyo kwa Kiswahili vinaitwa kifupi VVU ("Virusi vya UKIMWI"; kwa Kiingereza: HIV, yaani "Human Immunodeficiency Virus") na vinashambulia mwili kwa kuondoa nguvu zake za kupambana na maambukizi nyemelezi yanay... |
1901 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Desemba | Desemba | Desemba ni mwezi wa kumi na mbili katika kalenda ya Gregori na ni kati ya miezi saba katika kalenda hiyo yenye siku 31.
Tarehe 21 ya mwezi huo wa Desemba (katika miaka mingine inawezekana kuwa tarehe 20 au 22) ni siku ya solistasi ya Kusini (kutoka Kiingereza solstice), yaani wakati Jua linapokuwa kusini kabisa mwa I... |
1904 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mmea | Mmea | Mimea (kwa Kiingereza: "plants", kutoka Kilatini "Plantae") ni moja kati ya makundi ya viumbe hai duniani likijumuisha miti, maua, mitishamba na kadhalika. Kuna zaidi ya aina 300,000 ya mimea.
Sayansi inayochunguza mimea huitwa botania ambayo ni kitengo cha biolojia. Kwenye uainishaji wa kisayansi mimea hujumlishwa ka... |
1907 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Usanifu%20majengo | Usanifu majengo | Usanifu majengo ni sanaa na sayansi ya kubuni muundo na sura ya majengo. Sanaa na sayansi hii inajumuisha pia mambo kama mipango miji, usanifu wa eneo la kujenga, na hata ubunifu wa samani zitakazotumika ndani ya jengo.
Watu wanaojihusisha na haya huitwa "wasanifu majengo". Wanahitaji elimu ya ujenzi, hesabu, sanaa, t... |
1908 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mipango%20miji | Mipango miji | Mipango miji ni sayansi na sera kuhusu maendeleo ya kijamii, kiuchumi, kimazingira katika miji na vitongoji vyake. Mgiriki Hippodamus anasemekana kuwa ndiye baba wa mipango miji kutokana na ubunifu wake wa mji wa Miletus ingawa kumekuwa na miji iliyopangwa kabla yake.
Taaluma ya mipango miji imechipuka toka kwenye ta... |
1910 | https://sw.wikipedia.org/wiki/IRC | IRC | Internet Relay Chat (IRC) ni aina ya mawasiliano ya papo kwa hapo kupitia mtandao wa Intaneti. Teknolojia hii imeundwa hususan kwa ajili ya mawasiliano ya watu wengi kwa wakati mmoja, lakini pia mawasiliano ya mtu mmoja kwa mmoja yanawezekana.
Teknolojia hii ilitengenezwa na Jarkko Oikarinen Agosti 1998 ili kuchukua n... |
1911 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Blogu%20za%20mkononi | Blogu za mkononi | Blogu za mkononi ni aina ya blogu zinazotumia zana zinazoshikika mkononi kama vile simu za mkononi. Kwahiyo, habari, maoni, au visa vinatolewa katika mtandao wa kompyuta kwa kutumia zana hizi. Teknolojia hii ilianza huko Japan ambapo simu za mkono zenye kamera zilianza kupatikana kwa urahisi.
Inasemekana utumaji wa h... |
1912 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Paul%20Simon | Paul Simon | Paul Simon ni mwanamuziki wa country, anaimba na kupiga gitaa. Amewahi kushirikiana na wanamuziki wengi; moja ya makundi hayo ni Ladysmith Black Mambazo. Nyimbo alizowahi kuimba ni "Homeless", "Mother and child reunion" na "Diamond in the sole of her shoes".
Paul Simon alizaliwa tarehe 13 Oktoba 1941 katika mji wa New... |
1928 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Shaaban%20Robert | Shaaban Robert | Shaaban Robert (1 Januari 1909 - 22 Juni 1962) alikuwa mshairi na mwandishi wa riwaya. Mchango wake katika lugha ya Kiswahili ni mkubwa kwani kazi zake zinaheshimika katika fasihi ya Kiswahili na pia zinatumika shuleni.
Maisha
Shaaban Robert alizaliwa tarehe 1 Januari 1909 katika kijiji cha Vibambani, jirani na Machu... |
1930 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mbeya | Mbeya | Mbeya ni jina la:
Mji wa Mbeya
Mkoa wa Mbeya katika Tanzania Kusini-Magharibi
Wilaya za Mbeya mjini na vijijini
Jimbo Kuu la Mbeya la Kanisa Katoliki
Tanzania
Makala zinazotofautisha maana |
1950 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mbeya | Mkoa wa Mbeya | Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania, ukipakana na Zambia na Malawi, halafu na mikoa ya Rukwa, Tabora, Singida na Iringa, mbali na mkoa mpya wa Songwe uliomegwa kutoka ule wa Mbeya upande wa magharibi mwaka 2016. Una Postikodi namba 53000.
Kabla ya kugawiwa kulikuwa na wilaya 9 zifuatazo: Mbeya Mjini, Mbeya V... |
1951 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ladysmith%20Black%20Mambazo | Ladysmith Black Mambazo | Ladysmith Black Mambazo ni kundi la muziki ambalo linaimba bila kutumia ala za muziki. Kundi hili lipo Afrika ya Kusini. Neno "Mambazo" linamaanisha "shoka" kwa Kizulu. Na "Ladysmith" ni kitongoji katika jimbo la Natal alichotoka Joseph Shabalala kiongozi na mwanzilishi wa kundi hili.
Ladysmith Black Mambazo lina alba... |
1952 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Arusha | Arusha | Arusha ni neno la kutaja watu na mahali katika Tanzania kaskazini-mashariki:
Kabila la Waarusha
Mkoa wa Arusha
Wilaya ya Arusha
Mji wa Arusha ni makao makuu ya mkoa na wilaya, pia makao makuu ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki
Tanzania
Makala zinazotofautisha maana |
1953 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Arusha | Mkoa wa Arusha | Mkoa wa Arusha ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 23000, na ni wa pili kwa utajiri nchini.
Wakazi ni 2,356,255.
Eneo
Eneo lake ni km za mraba 34,526 zikiwemo km² 707 za maji ya ndani..
Umepakana na Kenya upande wa kaskazini. Mikoa ya jirani, kufuatana na mwendo wa saa, ni: Kilimanjaro, ... |
1954 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Deutsche%20Welle | Deutsche Welle | Redio Deutsche Welle (DW), au Sauti ya Ujerumani ni kituo cha Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani kwa ajili ya matangazo ya nje.
Kituo kimeanzishwa mw. 1953 kilitoa matangazo ya Kijerumani kwa ajili ya Wajerumani kote duniani kwa njia ya SW.
Leo (2005) kituo hutangaza kwa redio za SM na FM kwa lugha 30 halafu kwa TV k... |
1956 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilomita%20ya%20mraba | Kilomita ya mraba | Kilomita ya mraba (km²) ni kipimo cha eneo; eneo lenye upana na urefu wa kilomita moja
Msingi wake ni mita ya mraba (m²). Kilomita ya mraba hutumika kwa upimaji wa maeneo makubwa duniani kama mji, mkoa, nchi au dunia yote.
Kilometa 1 ya mraba (km²) ni sawa na:
eneo la mraba yenye urefu wa kilomita moja kila upande
... |
1958 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Usawa%20bahari%20wastani | Usawa bahari wastani | Usawa wa wastani wa maji ya bahari hutumika kama kipimo cha kulinganisha kimo cha mahali duniani toka usawa wa bahari. Hali halisi usawa wa bahari hubadilika kati ya mahali na mahali na muda hadi muda. Kwa hiyo kuna kadirio la wastani wa vipimo hivyo inayotumika kuwa usawa bahari wastani.
Kawaida hutumika katika sente... |
1959 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Alfu%20Lela%20U%20Lela | Alfu Lela U Lela | Kitabu cha Alfu Lela U Lela au Usiku Elfu na Moja (كتاب ألف ليلة وليلة kwa Kiarabu au هزار و یک شب kwa Kiajemi) ni mkusanyiko wa fasihi katika muundo wa visa kutoka Mashariki ya Kati.
Maandishi na historia yake
Visa hivi vinatokana na kitabu cha zamani cha Kiajemi kiitwacho Hazâr Afsâna (Visa vya Ngano Elfu Moja). In... |
1960 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Karne | Karne | Karne ni muda wa miaka mia moja. Karne 10 ni milenia moja. Inawezekana kugawa karne kwa miongo 10.
Neno hili limetokana na Kiarabu "ﻗﺮﻥ" linamaanisha kipindi cha miaka mia moja. Kwa kawaida karne si miaka 100 yoyote inayofuatana lakini kipindi kati ya miaka kama vile 1901-2000 au 1801-1900.
Karne inakwisha katika mw... |
1961 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ubuntu | Ubuntu | Ubuntu ni falsafa ya Kiafrika inayosisitiza mahusiano na ushirikiano wa jamii kama msingi wa maisha bora na amani katika jamii.
Falsafa hii inaonesha nafasi ya mtu katika jamii iliyomzunguka. Ushirikiano ni njia bora ya kuishi kama jamii kuliko ubinafsi.
Neno Ubuntu limetoka kwenye lugha za Kizulu na Kixhosa za Afri... |
1962 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Malik%20Zulu%20Shabazz | Malik Zulu Shabazz | Malik Zulu Shabazz (amezaliwa mwaka wa 1968 kwa jina la Paris Lewis) ni mwanasheria nchini Marekani na kiongozi wa kundi la New Black Panther Party for Self Defence.
Wanasiasa wa Marekani |
1963 | https://sw.wikipedia.org/wiki/New%20Black%20Panther%20Party%20for%20Self%20Defence | New Black Panther Party for Self Defence | New Black Panther Party for Self-Defense ni kundi la wanaharakati weusi wenye siasa kali na mwamko wa kimapinduzi nchini Marekani. Kundi hili lilianzishwa mwaka 1989 na mtangazaji wa redio, Aaron Michaels, huko Dallas, Texas. Mwanzoni kundi hili lilichukua jina la "Black Panther Party" ambalo lilikuwa ni jina la kund... |
1968 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bendera%20ya%20Tanzania | Bendera ya Tanzania | Bendera ya Tanzania ni ya mstatili unaokatwa pembe kwa pembe na kanda nyeusi yenye milia za njano kandokando.
Pembetatu ya juu ina rangi ya majani, pembetatu ya chini ni ya buluu.
Matumizi ya bendera inahifadhiwa chini ya sheria ya "The National Flag and Coat of Arms Act, 15-1971".
Historia ya bendera
Bendera hii im... |
1970 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jakaya%20Kikwete | Jakaya Kikwete | Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa rais wa nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu tarehe 21 Desemba 2005 hadi tarehe 5 Novemba 2015.
Asili
Amezaliwa 7 Oktoba 1950 katika kijiji cha Msoga, kata ya Lugoba, tarafa ya Msoga, jimbo la uchaguzi la Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo, mkoa wa Pwani.
Lugha ya mama ilikuwa Kikwer... |
1985 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jens%20Fink-Jensen | Jens Fink-Jensen | Jens Fink-Jensen (alizaliwa Copenhagen, Denmark, 19 Desemba 1956) ni mwandishi katika lugha ya Kidenishi katika nyanja mbalimbali kama vile semi za kawaida na mashairi. Vile vile yeye ni mpigapicha na mwandishi wa vitabu hasa vya muziki na nyimbo.
Alianza maisha yake kama mwandishi wa vitabu vya hadithi 4 Juni 1975 wa... |
1989 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Krismasi | Krismasi | Krismasi (pia Noeli) ni sikukuu ambayo Wakristo wengi husheherekea kuzaliwa kwake Yesu Kristo zaidi ya miaka 2000 iliyopita.
Kwa kawaida husheherekewa tarehe 25 Desemba katika Ukristo wa magharibi na tarehe 6 Januari katika ule wa mashariki.
Jina
Kwa Kiswahili kuna majina mawili ya kawaida kwa ajili ya sikukuu hii:... |
1991 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Kagera | Mto Kagera | Mto Kagera (kwa Kinyarwanda: Akagera) ni kati ya mito inayounda mto Nile, pia ni mto mkubwa kabisa wa kuingia ziwa la Viktoria Nyanza.
Unaanzia Burundi inapounganika mito ya Nyawarongo na Ruvuvu ikiendela km 400 hadi kuingia ziwa Viktoria.
Mto Kagera ukielekea kaskazini ni mpaka kati ya Tanzania na Rwanda; pale una... |
1992 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kagera | Mkoa wa Kagera | Mkoa wa Kagera kati ya mikoa 31 ya Tanzania ndio mkoa wa kaskazini-magharibi kabisa wenye postikodi namba 35000. Jina lake linatokana na mto Kagera.
Mkoa wa Kagera umepakana na Burundi, Rwanda na Uganda upande wa Magharibi na Kaskazini. Upande wa Kusini umepakana na mikoa mingine ya Tanzania ya Kigoma, Shinyanga na G... |
1993 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kagera | Kagera | Kagera ina maana mbalimbali:
Kagera ni mto katika Tanzania
Mkoa wa Kagera ni mkoa katika Tanzania.
Kagera (Ukerewe) ni kata ya wilaya ya Ukerewe kwenye mkoa wa Mwanza (Tanzania)
{maana}}
Makala zinazotofautisha maana |
1996 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu | Yesu | Yesu (kwa Kiebrania יֵשׁוּעַ, Yeshua, kifupisho cha יהושע, Yeoshua, yaani "Mungu anaokoa") alikuwa Myahudi mwanamume aliyeishi miaka 2000 hivi iliyopita (labda 6 KK - 30 BK).
Alizaliwa na bikira Maria kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, huko Bethlehemu ya Uyahudi. Maisha yake yalikuwa ya pekee kwa kuwa alifahamu vitu vingi... |
1997 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania | Azania | Azania (kwa Kigiriki: Ἀζανία) ni jina la kihistoria la sehemu mbalimbali za pwani ya Afrika ya Mashariki. Asili yake ni zamani za Waroma na Wagiriki wa kale kwa eneo lililokuwa la watu wa Lugha za Kikushi.
Mapokeo ya Waroma na Wagiriki wa Kale
Mara ya kwanza jina hili limepatikana katika mwandishi Mroma Plinio Mzee (G... |
2000 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola | Jumuiya ya Madola | Jumuiya ya Madola (jina la Kiingereza ni Commonwealth of Nations) inaunganisha nchi mbalimbali hasa Uingereza na nchi zilizokuwa koloni zake.
Umoja huu umeanzishwa mw. 1926 kama "Jumuiya ya Kibritania" (British Commonwealth) na kupewa jina lake la sasa tangu 1949. Inafuatana na Dola la Kibritania au Dola la Kiingereza... |
2002 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mzunguko%20wa%20Bahari%20Nyekundu | Mzunguko wa Bahari Nyekundu | Mzunguko wa Bahari Nyekundu (kwa Kiingereza: Periplous of the Erythrean Sea) ni kitabu cha mwongozo kwa ajili ya mabaharia kilichoandikwa mnamo mwaka 70 BK.
"Periplous" ni neno la Kigiriki linalomaanisha tendo la kuzunguka bara kupitia bahari kwa merikebu; "Bahari ya Eritrea" ni jina la kale kwa ajili ya Bahari ya Sh... |
2003 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Eritrea | Bahari ya Eritrea | Bahari ya Eritrea (kwa Kigiriki ερυθρά θάλασσα, erythrá thálassa) ni jina la kale la Bahari ya Shamu na Bahari Hindi. Neno "erythra" katika lugha ya Kigiriki inamaanisha rangi nyekundu ("thalassa" = bahari). Hivyo bahari ile iliitwa "Bahari Nyekundu" (linganisha Kiingereza "Red Sea"). Inasemekana ya kwamba jina hilo li... |
2004 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Shamu | Bahari ya Shamu | Bahari ya Shamu (kwa Kiingereza Red Sea; kwa Kiarabu البحر الأحمر Baḥr al-Aḥmar, al-Baḥru l-’Aḥmar; kwa Kiebrania ים סוף Yam Suf; kwa Kitigrinya ቀይሕ ባሕሪ QeyH baHri) ni ghuba kubwa ya Bahari ya Hindi. Jina la kihistoria katika lugha ya Kigiriki lilikuwa Bahari ya Eritrea (ερυθρά θάλασσα, erythrá thálassa).
Kaskazini k... |
2006 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar | Jamhuri ya Watu wa Zanzibar | Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingawa inajitawala katika mambo ya ndani.
Hadi mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 nchi hiyo ilijulikana kama Usultani wa Zanzibar.
Jina
Etimolojia ya Neno Zanzibar
Jiografia
Eneo lake ni sawa na funguvisiwa la Zanzibar lililopo mbele ya mwamb... |
2007 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami | Tsunami | Tsunami ni wimbi kubwa sana katika bahari linalosababishwa na tetemeko la ardhi, mlipuko wa volkano au matokeo mengine yanayoleta mshtuko wa ghafla chini ya maji. Mshtuko huo unasababisha kutokea kwa wimbi kali linaloanza kupaa juu likifika katika maji kame na kwenye ufuko wa bahari.
Neno tsunami linatokana na lugha y... |
2008 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Tanganyika%20African%20National%20Union | Tanganyika African National Union | Tanganyika African National Union (TANU) kilikuwa chama kilichotawala Tanganyika na Tanzania hadi muungano wa chama hiki na Chama cha Afro-Shirazi cha Zanzibar ulipounda Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977.
TANU ilianzishwa 7 Julai 1954 kutokana na Tanganyika African Association (TAA). TAA ilikuwa na mwelekeo wa kita... |
2009 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Benjamin%20Mkapa | Benjamin Mkapa | Benjamini William Mkapa (12 Novemba 1938 - 24 Julai 2020) alikuwa Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1995-2005) na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, CCM.
Wasifu
Mkapa alizaliwa Lupaso karibu na Masasi katika kusini-mashariki ya Tanganyika. Kuanzia 1945 hadi 1951 alsoma shule za msingi pale Lup... |
2010 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Reli%20ya%20Kenya-Uganda | Reli ya Kenya-Uganda | ''Makala hii yaeleza habari za njia ya reli ya kihistoria kati ya Mombasa na Uganda. Kwa habari za Shirika ya Reli ya Uganda ya kisasa tazama Uganda Railways Corporation.
Reli ya Kenya-Uganda ni jina kwa reli kati ya Mombasa na Kampala iliyojengwa na Waingereza kuanzia mwaka 1896. Mwanzoni ilijulikana kwa jina la "Rel... |
2011 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Port%20Bell | Port Bell | Port Bell ni mji mdogo karibu na Kampala/ Uganda ufukoni wa ziwa la Viktoria Nyanza. Jina la mji limetokana na Sir Hesketh Bell aliyekuwa kamishna (gavana) Mwingereza huko Uganda kuanzia mwaka. 1905-1909.
Port Bell ni bandari kwa ajili ya Kampala. Feri zinatoka kwenda Jinja, Kisumu na Mwanza.
Kuna viwanda kadhaa kam... |
2012 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad | Chad | Chad (pia: Chadi) ni nchi huru iliyoko Afrika ya Kati. Imepakana na Libya, Sudan, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Kamerun, Nigeria na Niger.
Mji mkuu ni Ndjamena.
Jiografia
Sehemu kubwa ya eneo lake ni jangwa na nchi yabisi. Kusini kuna kanda lenye hali ya hewa ya kitropiki, lakini ardhi yenye rutuba inayofaa kwa kilimo... |
2016 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Athi | Athi | Athi ni jina la mto katika kaunti ya Kitui, Kenya, Afrika Mashariki. Sehemu za mto hujulikana pia kwa majina ya Galana na Sabaki, kwa hiyo mto wote huitwa pia Athi-Galana-Sabaki.
Ina urefu wa kilomita 390, na beseni lenye eneo la Km² 70,000.
Mto wa Athi umeupatia jina lake mji wa Athi River karibu na Nairobi pia kwa ... |
2017 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf | Ludwig Krapf | Johann Ludwig Krapf (11 Januari 1810 – 26 Novemba 1881) alikuwa mmisionari wa kwanza wa Uprotestanti nchini Kenya katika karne ya 19 akatunga kamusi ya kwanza ya lugha ya Kiswahili.
Masomo Ujerumani na Uswisi
Krapf alizaliwa tarehe 11 Januari 1810 katika kijiji cha Derendingen karibu na Tübingen, eneo la Württemberg,... |
2018 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori | Komori | Komori (kwa Kiswahili pia: Visiwa vya Ngazija; kwa Kikomori: قمر, Komori, kwa Kifaransa: Comores) ni nchi huru kwenye funguvisiwa katika Bahari Hindi upande wa Mashariki wa Afrika. Iko katika Kanali ya Msumbiji kaskazini kwa Madagaska na mashariki kwa Msumbiji.
Jina limetokana na lugha ya Kiarabu ambapo Juzur al-Qama... |
2021 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta | Jomo Kenyatta | Jomo Kenyatta (1893-1978) alikuwa rais wa kwanza wa Kenya.
Jina lake halisi lilikuwa Johnstone Kamau wa Ngengi. Alipewa jina la utani ambalo ni Mkuki wa Moto (Burning Spear). Jina la Kenyatta lilitokana na mkanda aliopenda kuuvaa ambao ulitengenezwa kwa shanga. Wagĩkũyũ wanauita kenyaata.
Maisha
Alisoma katika shule ... |
2022 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanza%20%28sarafu%29 | Kwanza (sarafu) | Kwanza (kifupi: KZ) ni pesa inayotumika kwa malipo halali katika nchi ya Angola.
Wakati wa uhuru Angola ilirithi pesa ya escudo kutoka Ureno. Mwaka 1977 Kwanza yenye Lwei 100 imeingizwa nchini kama pesa ya kwanza ya kitaifa. Kutokana na kushuka kwa thamani ya fedha mara kwa mara pesa ya Kwanza imebadilishwa mara nne ... |
2023 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanzaa | Kwanzaa | Kwanzaa ni sikukuu inayosherehekewa kati ya Wamarekani Weusi nchini Marekani kwa muda wa siku saba toka tarehe 26 mwezi wa disemba hadi tarehe 1 mwezi wa Januari. Sikukuu hii ilianzishwa Kalifornia na Maulana Ron Karenga tarehe 26 Diesemba mwaka 1966.
Karenga alitunga neno jipya "Kwanzaa" kutokana na neno la Kiswahil... |
2024 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Visa%20vya%20Esopo | Visa vya Esopo | Visa vya Esopo vinatokana na masimulizi ya Esopo, ambaye inaaminika kuwa alikuwa ni mtumwa wa Kiafrika aliyeishi kati ya mwaka 620 na 560 Kabla ya Kristo katika Ugiriki wa Zamani. Visa vyake hutumiwa kutoa mafunzo na kuburudisha. Visa hivi hutumiwa kwa wingi katika vitabu vya watoto na vikaragosi.
Historia ya Esopo... |
2026 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Guinea | Guinea | Guinea (pia: Gine, Gini) ni nchi katika Afrika ya Magharibi. Pengine inatajwa kama Guinea-Conakry ili kuitofautisha na nchi za Guinea-Bissau na Guinea ya Ikweta.
Imepakana na Guinea-Bisau, Senegal na Mali upande wa kaskazini, Côte d'Ivoire, Liberia na Sierra Leone kusini halafu Bahari Atlantiki upande wa magharibi.
E... |
2027 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas | Abu Nuwas | Abu Nuwas (kwa Kiarabu أبو نواس) alikuwa mshairi Mwarabu aliyeishi 760-815. Katika utamaduni wa Kiswahili ni jina la mhusika katika hadithi za “Hekaya za Abunuwasi”.
Maisha
Mshairi Abu Nuwas alizaliwa Ahwaz (Irak). Mama yake alikuwa Mwajemi na baba alikuwa mwanajeshi Mwarabu ambaye hakupata kumjua. Jina lake halisi l... |
2032 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Bi%20Kidude | Bi Kidude | Bi Kidude (jina halisi: Fatuma binti Baraka; amefariki Bububu, Zanzibar, 17 Aprili 2013, akikisiwa kuwa na umri wa miaka 102) alikuwa gwiji wa muziki katika bara la Afrika. Bi Kidude alikuwa msanii mkongwe na mahiri sana katika fani ya muziki wa mwambao ambao hujulikana kwa jina la Taarabu. Muziki huo, ambao ni mchanga... |
2033 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Binyavanga%20Wainaina | Binyavanga Wainaina | Binyavanga Wainaina (18 Januari 1971 - 21 Mei 2019) alikuwa mwandishi kutoka nchini Kenya.
Maisha
Alizaliwa Nakuru, nchini Kenya. Alihudhuria masomo ya msingi na sekondari nchini Kenya kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Transkei, Afrika Kusini.
Baada ya kumaliza masomo yake alihamia katika jiji la Cape Town ambapo ... |
2035 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkutano%20huria | Mkutano huria | Mkutano huria ni mkutano ambao unaendeshwa na wahudhuriaji au wajumbe badala ya mwandaaji au waandaaji wa mkutano. Katika mkutano wa aina hii hakuna watoa mada na wapokea mada, hakuna watoa hotuba na wasikilizaji. Wahudhuriaji wote ndio watoa mada na wapokea mada. Dhana hii imepewa umaarufu na wataalamu wawili wa progr... |
2036 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Podikasiti | Podikasiti | Podikasiti ni neno lililoanza kutumiwa mwaka 2004 pale matumizi ya programu ya RSS ilipoanza kutumiwa kusambaza matangazo kwa ajili ya kusikiliza kupitia tarakilishi au zana nyingine za mkononi kama vile aipodi.
Podikasiti ni mafaili ya video au sauti ambayo yako kwenye mtandao wa tarakilishi kwa ajili ya yeyote yule... |
2042 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Singida | Mkoa wa Singida | Mkoa wa Singida ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania: mkoa huu upo kanda ya kati, ukipakana na mikoa ya Manyara upande wa kaskazini , Dodoma mashariki, Iringa, Mbeya kusini, Tabora upande wa magharibi na Shinyanga. msimbo wa posta ni 43000.
Kuna wilaya sita za Iramba, Manyoni, Singida Vijijini na Singida Mjini, Ikungi na M... |
2044 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kigermanik | Kigermanik | Lugha za Kigermanik ni kikundi cha lugha zenye asili ya Ulaya ya Kaskazini.
Lugha za Kigermanik zenye wasemaji wengi ni Kiingereza (milioni 380) na Kijerumani (milioni 120). Lugha nyingine za Kigermanik ni lugha za Skandinavia, halafu Kiholanzi na Kiafrikaans wa Afrika Kusini.
Historia
Mwanzo wa lugha hizi uko gizan... |
2048 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Uganda | Uganda | Uganda ni nchi ya Afrika ya Mashariki. Imepakana na Kenya upande wa mashariki, Sudan Kusini upande wa kaskazini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa magharibi, Rwanda na Tanzania upande wa kusini.
Uganda inamiliki sehemu ya ziwa la Viktoria Nyanza ikipakana huko na Kenya na Tanzania.
Uganda ni nchi mwanachama... |
2050 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Iringa | Mkoa wa Iringa | Mkoa wa Iringa ni mojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 51000. Upo katikati ya nchi, kidogo upande wa kusini. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Njombe, Mbeya, Singida na Dodoma.
Makao makuu yako katika manisipaa ya Iringa.
Jiografia
Mkoa wa Iringa uko katika Nyanda za Juu za Kusini mwa ... |
2055 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Dar%20es%20Salaam | Mkoa wa Dar es Salaam | Dar es Salaam ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepakana na Mkoa wa Pwani pande zote barani na Bahari ya Hindi upande wa mashariki.
Eneo la mkoa ni jiji la Dar es Salaam ambalo ndilo kitovu cha shughuli za biashara (na za utawala, kwa kiasi fulani) nchini Tanzania, na ni kati ya majiji yanayokua haraka zaidi duniani.... |
2059 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Dodoma | Mkoa wa Dodoma | Mkoa wa Dodoma ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 41000. Uko katikati ya nchi na umepakana na mikoa ya Manyara, Morogoro, Iringa na Singida.
Eneo lote la mkoa lina km² 41,310. Sehemu kubwa ni nyanda za juu kati ya mita 830 hadi 2000 juu ya UB.
Katika sensa ya mwaka 2022, idadi ya wakazi wa Mkoa w... |
2060 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiyunani | Kiyunani | Kiyunani ni jina la Kiswahili cha zamani kwa "Kigiriki", ambayo ni lugha ya nchi ya Ugiriki ("Uyunani") au kwa tabia za Wagiriki ("Wayunani").
Neno la Kiswahili cha zamani limetokana na lugha ya Kiarabu ambapo يونان yunan linataja kiasili Wagiriki wa eneo la Ionia au wa kabila la Waioni walioishi kwenye pwani ya masha... |
2062 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma%20%28maana%29 | Roma (maana) | Roma (pia: Rumi) ni jina linalotumika kwa mji wa Roma (mji mkuu wa Italia), ama kwa dola la Roma lililokuwa kwa karne kadhaa kabla na baada ya Kristo dola kubwa kuliko zote duniani, tena kwa Kanisa la Roma ambalo ni kiini cha Kanisa Katoliki lote. Lilikuwa pia jina la mungu wa kike katika dini ya Roma ya Kale.
Roma a... |
2064 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilatini | Kilatini | Kilatini ni lugha ya kihistoria ambayo siku hizi haina tena wasemaji kama lugha ya kwanza, lakini bado hufundishwa katika shule, vyuo na hata kutumiwa kama lugha ya pili. Ilikuwa pia lugha ya kimataifa ya elimu na hata leo istilahi nyingi za kisayansi zimetoka katika Kilatini.
Historia
Kilatini kilikuwa lugha hai tak... |
2066 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Zambia | Zambia | Jamhuri ya Zambia ni nchi ya Kusini mwa Afrika isiyo na mwambao baharini.
Imepakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Tanzania upande wa kaskazini, Malawi upande wa mashariki, Msumbiji, Zimbabwe na Botswana upande wa kusini, Namibia na Angola upande wa magharibi.
Mji mkuu ni Lusaka (wenye wakazi 1,747,152 mwaka... |
2069 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Tabora | Mkoa wa Tabora | Mkoa wa Tabora ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 45000.
Makao makuu yako Tabora Mjini. Tabora ni jina la mji, wilaya na mkoa wa Tanzania ya kati.
Eneo la mkoa ni km2 76,151; mnamo km2 34,698 (46%) ni hifadhi ya misitu, km2 17,122 (22%) ni hifadhi ya wanyama.
Jumla ya wakazi ilikuwa watu 3,391,... |
2072 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Morogoro | Mkoa wa Morogoro | Morogoro ni jina la mto, mji, wilaya na mkoa wa Tanzania.
Mkoa wa Morogoro ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 67000. Umepakana na mikoa ya Tanga, Pwani, Lindi, Ruvuma, Iringa, Dodoma na Arusha.
Eneo lake ni km² 72 939, ambapo kuna wakazi 3,197,104 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 (kutola 2,218,492 w... |
2073 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Morogoro | Morogoro | Morogoro ni jina la>
Mto Morogoro
Mji wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro
na Wilaya za Morogoro Mjini na Morogoro Vijijini.
Tanzania
Makala zinazotofautisha maana |
2080 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Michael%20Jackson | Michael Jackson | Michael Joseph Jackson (29 Agosti 1958 – 25 Juni 2009) alikuwa mwimbaji, dansa na mburudishaji kutoka nchini Marekani. Hufahamika zaidi kwa jina la kiheshima-utani kama Mfalme wa Pop. Hutambulika kama mburudishaji aliyepata mafanikio zaidi kwa muda wote, na moja kati ya waburudishaji wenye mvuto na athira kubwa katika ... |
2081 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mnazi | Mnazi | Mnazi ni neno linaloweza kutaja:
mti wa mnazi (mti) mwenye matunda ya nazi
kinywaji cha mnazi (kinywaji) kinachotengenezwa na utomvu wa nazi changa
Makala zinazotofautisha maana |
2086 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinywaji | Kinywaji | Kuna vinywaji vingi:
Maji
Chai
Kahawa
Maziwa
Soda
Togwa
Maji ya matunda
Pombe
Mnazi
Mvinyo
Mbege
Bia
Kimpumu
Chang'aa |
2087 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Swala | Swala | Kwa swala kama ibada ya Kiislamu, taz. Swalah.
Swala ni wanyama walao nyasi katika nusufamilia Antilopinae, Aepycerotinae na Pantholopinae za familia Bovidae. Hupatikana katika maeneo yenye nyasi fupi fupi na vichaka vifupi fupi hasa kwenye maeneo mengi ya hifadhi katika Afrika. Spishi nyingine hukimbia kilometa 80 kw... |
2088 | https://sw.wikipedia.org/wiki/John%20F.%20Kennedy | John F. Kennedy | John Fitzgerald Kennedy (29 Mei 1917 – 22 Novemba 1963) alikuwa Rais wa Marekani kuanzia mwaka 1961 hadi alipouawa.
Maisha
Alikuwa mtoto wa pili katika familia ya watoto 9. Baba yake alikuwa mfanyabiashara maarufu wa ukoo wenye asili ya Eire.
Vita Kuu ya Pili ilipoanza alijiunga na jeshi la wanamaji. Mwaka 1943 alij... |
2097 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwarara | Kwarara | Kwarara ni ndege wa nusufamilia Threskiornithinae katika familia Threskiornithidae ambao wana miguu mirefu. Domo refu lao limepindika na hutumika kwa kutafuta chakula ndani ya matope. Spishi nyingi za kwarara huweka matago yao juu ya miti, kwa kawaida pamoja na yange, koikoi au domomwiko. Jike huyataga mayai 2-4.
Spis... |
2099 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Alexander%20Graham%20Bell | Alexander Graham Bell | Alexander Graham Bell (3 Machi 1847 – 2 Agosti 1922) alikuwa kati ya wagunduzi wa mawasiliano ya simu. Alizaliwa katika mji wa Edinburgh nchini Uskoti lakini baadaye alihamia nchi za Kanada na Marekani. Baba yake alikuwa mwalimu wa watoto wenye matatizo ya kusikia na kuongea. Alifanikiwa katika jaribio lake la kwanza m... |
2100 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Karl%20Friedrich%20Benz | Karl Friedrich Benz | Karl Friedrich Benz alizaliwa tar. 25 Novemba 1844 akiitwa Karl Friedrich Michael Vaillant huko Mühlburg / Karlsruhe Ujerumani wa Kusini Magharibi. Baada ya kumzaa mamake Josephine Vaillant akaolewa na babake Johann Georg Benz. Hivyo akaitwa Karl Friedrich Michael Benz lakini baadaye akajiita Carl Friedrich Benz.
Alik... |
2106 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Isaac%20Newton | Isaac Newton | Isaac Newton (25 Desemba 1642 – 20 Machi 1727) alikuwa mwanahisabati, mwanafizikia na mwanateolojia kutoka nchi ya Uingereza.
Anakumbukwa duniani kote kutokana na michango yake mbalimbali katika sayansi.
Ndiye aliyegundua tawi la kalkulasi (sambamba na Leibniz), sheria za mwendo na ya uvutano (graviti).
Mchango m... |
2108 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Marko | Mtakatifu Marko | Mtakatifu Marko (kwa Kilatini Mārcus; kwa Kigiriki Μᾶρκος) aliishi katika karne ya 1 BK. Alikuwa Myahudi wa Yerusalemu aliyeongokea mapema Ukristo pamoja na Maria mama yake. Kanisa la kwanza lilikuwa linakusanyika nyumbani mwao.
Alifanya kazi na mitume Paulo na Barnaba katika kuhubiri Injili huko Kupro na Uturuki wa l... |
2109 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo | Mtakatifu Paulo | Mtume Paulo (7-67 hivi) ni mmisionari mkuu wa Yesu Kristo katika historia ya Kanisa.
Alitangaza kifo na ufufuko wake katika nchi karibu zote zilizopo kaskazini kwa Bahari ya Kati.
Alimaliza ushuhuda wake kwa Yesu kwa kufia dini yake mjini Roma wakati wa dhuluma iliyoanzishwa na Kaisari Nero.
Tangu kale anaheshimiwa ... |
2116 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo | Baada ya Kristo | Baada ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo (kifupi: BK) ni namna ya kutaja miaka ambayo imekuwa njia ya kuhesabu miaka inayotumika zaidi duniani.
Kila mwaka huhesabiwa kuanzia ule uliodhaniwa kuwa mwaka wa kuzaliwa kwake Yesu Kristo. Miaka iliyotangulia kuzaliwa kwake Yesu huitwa Kabla ya Kuzaliwa kwake Yesu Kristo au kifup... |
2117 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Milenia | Milenia | Milenia (kutoka neno la Kiingereza millennium, ambalo mizizi yake ni katika Kilatini: mille, elfu, na annus, mwaka) ni kipindi cha miaka elfu moja.
Hii ni sawa na kusema milenia ina karne kumi.
Kwa sasa tuko katika milenia ya pili BK iliyoanza tarehe 1 Januari 2001. Lakini watu wengi walisheherekea tarehe 1 Januari ... |
2118 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari | Kaizari | Kaizari ni cheo cha mfalme mkuu. Neno la Kiswahili limetokana na lugha ya Kijerumani "Kaiser", lakini asili yake ni Kilatini "Caesar".
Asili ya Kiroma
Asili ya cheo ni Julius Caesar aliyekuwa kiongozi wa Dola la Roma hadi kuuawa kwake na wapinzani mwaka 44 KK.
Watawala waliomfuata walianza kutumia jina la Caesar kwa... |
2119 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Duma | Duma | Duma ni mnyama mbuai aliyemo katika jamii ya paka (Felinae) ambaye hupatikana Afrika na kidogo sehemu za Asia. Chakula chake ni wanyama jamii ya swala .
Kichwa chake ni kidogo zaidi ukilinganisha na wanyama wengine wa jamii yake kama chui. Duma anatofautiana na chui pia kwa sehemu ya mgongo na sehemu ya machoni: mgo... |
2120 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra | Hijra | Hijra (هجرة) ni neno la Kiarabu linalomaanisha tendo la Mtume Muhammad la kutoka Makka na kuhamia Madina mwaka 622 BK. Mwaka huo umekuwa tarehe ya kuanzisha kalenda ya Kiislamu ambayo miaka yake huhesabu miaka baada ya hijra.
Maana asili ya neno lenyewe ni "kuachana" au "kutengana", kutokana na historia ya Muhammad li... |
2121 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler | Adolf Hitler | Adolf Hitler (Braunau, Austria, 20 Aprili 1889; Berlin, Ujerumani, 30 Aprili 1945) alikuwa dikteta wa Ujerumani kuanzia mwaka 1933 hadi kifo chake.
Alihutubia dharau na chuki ya kimbari dhidi ya watu wote wasio Wagermanik na hasa dhidi ya Wayahudi. Alisababisha Vita Kuu ya Pili ya Dunia na mateso ya watu milioni kadh... |
2122 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra | Miaka baada ya hijra | Miaka baada ya Hijra ni hesabu ya miaka katika kalenda ya Kiislamu.
Hesabu hii ilianzishwa miaka 17 baada ya tukio lenyewe (638 BK) kufuatana na azimio la Khalifa Umar ibn al-Khattab.
Waarabu waliwahi kuwa na kalenda iliyotumia mwendo wa mwezi lakini hawakuhesabu miaka. Kila mwaka ulitajwa kutokana na tukio fulani.... |
2127 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu | Kalenda ya Kiislamu | Kalenda ya Kiislamu ni mtindo wa kuratibu wakati unaopatikana katika nchi mbalimbali za Kiislamu. Tofauti na kalenda ya kawaida inayofuata jua hii ni kalenda ya mwezi inayofuata kuandama kwa mwezi.
Pia Waislamu wanaoishi katika mazingira yasiyo ya Kiislamu hutumia kalenda hii kwa ajili ya kupanga maisha yao ya kidini,... |
2128 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi | Mkoa wa Lindi | Lindi ni jina la mji, wilaya na mkoa ulioko Kusini-Mashariki mwa Tanzania.
Mkoa wa Lindi ni kati ya mikoa 31 iliyopo nchini Tanzania yenye postikodi namba 65000.
Umepakana na mikoa ya Pwani, Mtwara, Ruvuma na Morogoro. Upande wa mashariki hupakana na Bahari Hindi.
Eneo la mkoa
Mkoa huu umeanzishwa mwaka 1971 na una ... |
2131 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilwa | Kilwa | Kilwa ni jina la wilaya na mahali patatu katika mkoa wa Lindi, Tanzania.
Wilaya ya Kilwa iko kati ya Dar-es-salaam na Lindi ufukoni wa Bahari Hindi.
Kilwa Masoko ni makao makuu ya wilaya.
Kilwa Kivinje ni mji wa kihistoria tangu karne ya 18.
Kilwa Kisiwani ni kisiwa karibu na mwambao kinachotazama Kilwa Masoko. Ha... |
2135 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Keremkerem | Keremkerem | Keremkerem ni ndege wa familia ya Meropidae. Wana mwili mwembamba wa rangi maridadi. Mdomo wao ni mrefu na mwembamba na mkia wa aina nyingi za keremkerem una mileli mirefu katikati.
Ndege hao wanaishi uwandani kwa kanda ya tropiki na nusu-tropiki ya Afrika, Ulaya na Asia. Hula wadudu, nyuki, manyigu na mabunzi hasa, a... |
2137 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Pangani%20%28mto%29 | Pangani (mto) | Kwa matumizi mengine ya jina hili angalia hapa Pangani
Mto Pangani ni kati ya mito mikubwa ya Tanzania. Unabeba maji ya Milima ya Meru, Kilimanjaro, Pare na Usambara kwenda Bahari ya Hindi. Mdomo wake uko mjini Pangani.
Jina
Mto unapita katika maeneo ya jumuiya zenye lugha tofautitofauti, hivyo kuna majina mbalimba... |
2138 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Rhapta | Rhapta | Rhapta ni jina la soko na mji wa kale katika pwani la Afrika ya Mashariki. Habari zake zilipatikana tangu karne ya kwanza katika mwongozo wa kigiriki kwa ajili ya mabaharia. Jina la Rhapta lilitajwa tena katika vitabu vingine hadi karne ya 6 BK lakini baadaye lilipotea au kubadilishwa.
Wataalamu walio wengi hukubalia... |
2140 | https://sw.wikipedia.org/wiki/Pangani%20%28mji%29 | Pangani (mji) | Pangani ni mji wa Mkoa wa Tanga, nchini Tanzania, uliopo ufukoni mwa Bahari Hindi kati ya Dar es Salaam na Tanga ukielekea pande zote mbili za mdomo wa mto Pangani.
Leo hii ni mji mdogo mwenye wakazi karibu 8n000 na makao makuu ya Wilaya ya Pangani. Lakini ina historia ndefu, hasa kwa sababu kuna bandari nzuri ya kia... |
2141 | https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Tyndale | William Tyndale | William Tyndale alikuwa mwanatheolojia Mwingereza, kasisi ya kanisa na mtaalamu aliyetafsiri Biblia mara ya kwanza katika Kiingereza cha kisasa. Alizaliwa huko Gloucestershire mnamo mwaka 1494 - aliuawa Vilvoorde (Brabant - Ubelgiji ya leo) tarehe 6.9.1536. Tafsiri yake ya Biblia ilikuwa toleo la kwanza lililochapishwa... |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.