text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
Rai hiyo ilitolewa juzi katika Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, na mkaguzi wa viwanda vya pamba mwandamizi, Kisinza Ndimu, kwenye semina ya ubora na usafi wa pamba, kwa wanunuzi wa pamba mbegu ngazi ya vituo, iliyofanyika katika ukumbi wa kiwanda cha kampuni ya Oram LTD mijini Bunda.Ndimu alisema wakulima na wanunuzi wa zao hilo wamekuwa wakiharibu kwa makusudi ubora na usafi wa zao la pamba, hali ambayo imekuwa ikisababisha thamani yake kushuka kila mwaka.Alisema wanunuzi wamekuwa wakifanya uharibifu huo kwa asilimia zaidi ya 80 wakati inapofika katika vituo vyao vya kununulia pamba na akayataka makundi yote mawili, pamoja na wadau mbalimbali kuzingatia ubora na usafi wa zao hilo.“Watu wamekuwa wakiharibu kwa makusudi kabisa ubora na usafi wa zao la pamba, wanaweka maji, mchanga na vitu vingine ambavyo havifai kabisa ili kushusha ubora, ” alisema Ndimu.Ofisa mwandamizi wa zao la pamba nchini, Emily Mbagulle, alisema ni jukumu la kila mdau wa zao la pamba, kuzingatia ubora wa zao hilo, kuanzia wakati wa kuandaa shamba, kulima, kuvuna, kuhifadhi, pamoja na wakati wa kuuza ili kuimarisha uboa wake.“Hili ni jukumu letu sote kuhakikisha tunalinda na kuimaraisha ubora wa zao la pamba maana wote tunalitegemea zao hili,” alisema.Akichangia hoja katika semina hiyo Meneja wa kiwanda cha Oram Tanzania LTD, Dick Chiriwo, kilichoko wilayani Bunda, aliwahasa wanunuzi wa zao hilo, kujenga mshikamano wa pamoja kwa kuacha kununua pamba ambayo haina ubora, kwa lengo la kupata pamba nyingi maana hiyo itakuwa ni hasara kwao.“Wote wanunuzi mkishakamana na kukataa kabisa kununua pamba chafu mtakomesha hali hii….sasa unakuta mwingine anakataa kununua pamba chafu lakini mwingine wa sehemu hiyo hiyo anaikimbilia eti aweze kupata pamba nyingi, hiyo ni hasara kwenu acheni kabisa na wote mshikamane,” alisema Chiriwo.Baadhi ya wanunuzi wa zao hilo wakiwemo wakulima na wanunuzi walisema kuwa kuna changamoto nyingi zinazowakabili wakulima, ikiwa ni pamoja na ya kutokupata pembejeo kwa wakati, pamoja na kupewa dawa za kuua wadudu ambazo hazina uwezo, pamoja na mbegu ambazo hazioti.
5
TANZANIA na Uganda zimeeleza kuwa mipango ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda mpaka Tanga,Tanzania, inatarajia kukamilika mwakani.Hali hiyo inatokana na hatua ya Uganda, kubadili muda wa uzalishaji kutoka Desemba 2020 hadi katikati ya mwaka 2021. Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kapuulya Musomba aliliambia gazeti hili kuwa Tanzania inaendelea kufanya kazi kwa pamoja na serikali ya Uganda na wawekezaji, kuhakikisha mradi unakamilika kwa muda uliokadiriwa.Alisema kwa sasa wanafanya kazi na wawekezaji wa bomba hilo, watakamilisha masuala mengi ya uwekezaji ifikapo mwishoni mwaka huu na shughuli za ujenzi zitaanza katika robo ya kwanza ya mwaka 2019.“Baada ya majadiliano ya wadau kukamilika na makubaliano kuidhinishwa, TPDC inatarajia kuwekeza kwa niaba ya serikali katika robo ya kwanza ya mwaka ujao. “Taratibu zingine ziko katika ngazi mbalimbali za maamuzi kuhakikisha nia na lengo kwa nchi mbili na wawekezaji kwa upande mwingine zinakuwa na mafanikio,” alisema.Wiki iliyopita Benki ya Stanbic Uganda, imeongoza kuwezesha mipango ya kupata dola bilioni 2.5 kwa ajili ya bomba hilo la mafuta la kilometa 1,455, linalojulikana kama bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).Waziri wa Nishati nchini Uganda, Irene Muloni, akizungumza katika Mkutano wa Wiki ya Mafuta Afrika uliofanyika Cape Town, Afrika Kusini wiki iliyopita, alisema mazungumzo yaliyochukua muda mrefu ya wawekezaji, yamefanya serikali kubadili muda wa kuanza uzalishaji wa mafuta na kufikiria kuanza 2021. Uganda imepokea michoro ya usanifu (FEED) Desemba mwaka jana na imechelewa kuithibitisha, kama ilivyokuwa imeahidi awali.Mazungumzo kwa ajili ya makubaliano ya kifedha, yanaendelea. “Kama ilivyo, tunasubiri kampuni kufanya maamuzi ya mwisho kuhusu uwekezaji kwani michoro tayari imekamilika,” alisema.Muloni alisema kwa sasa wako kwenye mchakato wa kuidhinisha michoro, kwani ripoti ya tathmini ya mazingira na athari kwa jamii iko katika hatua za mwisho na wanatarajia kuikabidhi kwa serikali mwezi ujao kwa ajili ya mapitio.Alisema watawasilisha ripoti kwa Baraza la usimamizi wa Mazingira mwezi ujao kwa kuithibitisha huku Meneja wa Kampuni ya Total anayeshughulikia masuala ya jamii na Ardhi, Jean Lennock, aliongeza kuwa wanatarajia kutoa cheti cha ESIA baada ya ripoti kuidhinishwa.Idhini hiyo inatarajia kupatikana kabla ya mwisho wa robo ya kwanza ya mwaka ujao, hata kama Uganda na wadau wake wa mafuta, French Total E&P na China’s CNOOC, wanatarajia pia kufikia makubaliano ya mwisho ya uwekezaji kabla ya Juni. Tanzania na Uganda wanatarajia majadiliano ya serikali baina ya wanahisa hao wawili katika robo ya kwanza ya mwakani na kutoa makubaliano ya ndani ya kila serikali.“Tangu kuanza majadiliano Agosti mwaka jana tunaenda vizuri. Tupo ukingoni mwa majadiliano na tuanatarajia kumaliza kabla ya mwisho wa mwezi Machi,” alisema. Uganda, Tanzania na kampuni za mafuta, kwa miezi 18 wamekuwa wakifanyia kazi suala la fedha. Inaonekana kuwa nchi hizo mbili asilimia 70 ya mradi inategemea kutoka kwa wakopeshaji wa kimataifa. Asilimia 30 iliyobaki inatolewa kwa usawa na kampuni za Total, Tullow, CNOOC na JV na TPDC na Kampuni ya Taifa ya Mafuta Uganda.
3
Walisema, wakulima wengi hawana uelewa wa kutosha kuhusu thamani ya fedha hizo za kigeni na ndiyo sababu wanapohitaji kuzitumia inakuwa vigumu kwao, jambo linalowalazimu kuwatafuta watu waliosoma ambao nao huhitaji fedha ili kuwasaidia.Hali hiyo, inatokana na wakulima wengi kutofahamu mabadiliko ya fedha za kigeni zinazolipwa na makampuni yanayonunua tumbaku na mazao mengine ya wakulima yanayozalishwa kwa wingi katika wilaya hiyo.Mmoja wa wakulima wa kijiji cha Matepwende, Abdallah Ngonyani alisema, makampuni kutumia fedha za kigeni, hususan Dola kuwalipa wakulima ni sawa na kuwaibia kwa kuwa wakulima wengi wanaoishi maeneo ya mashambani huwa hawaji na kiwango cha kubadilisha fedha cha wakati huo.Mbali na hilo alisema huchukua muda mrefu hadi kufika mjini kufuata huduma za kibenki. Ni kwa msingi huo aliiomba Serikali kuanzia msimu huu wa 2015/2016 ikomeshe hali hiyo kwani inawarudisha nyuma wakulima wengi.Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ali Mpenye alisema, tayari ofisi yake imeshawaandikia barua watendaji wa vijiji na kata kuwajulisha kwamba hakuna anayeruhusiwa kununua mazao kutoka kwa wakulimakwa kutumia fedha za kigeni.
5
KLABU ya Simba itakuwa inapata kitita cha sh milion 900 kwa mwaka baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili na Kampuni ya Romario Sport kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya mazoezi na kuuza jezi za timu hiyo kwa msimu ujao. Mkataba huo unathamani ya Sh.milion 600 ndani ya kipindi cha miaka hiyo miwili, ambapo kila msimu timu hiyo itakuwa inavuna sh milion 300, pia watakuwa wakipata vifaa vya mazoezi pamoja na jezi za vyenye thamani ya sh milioni 200 kila msimu mpya ikiwa ni nje ya mktaba. Aidha watakuwa wanavuna mkwanja wenye thamani ya Sh.Milioni 100 kila mwaka ikiwa ni bonasi baada ya kampuni hiyo kufanya mauzo kwa mwaka. Mkataba huo unaotajwa kuwa mkubwa kusaini na timu hiyo ikilinganishwa huko nyuma ambapo walikuwa wakiingia gharama kubwa wakitoa kiasi cha milioni 120 ya kununua vifaa, utakuwa unaboreshwa mwaka hadi mwaka.Romario yenye makao makuu Dubai, itakuwa inauza bidhaa hizo za Simba nchini Tanzania kupitia wakala wao Kampuni ya Uhlsport ambao wanazambaza na kuuza pia jezi za timu ya Tanzania, Taifa Stars. Akizungumza jana wakati wanatia saini mkataba huo, Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori alisema mkataba huo unamanufaa mara mbili kwa Simba baada ya kupata shida kwa muda mrefu sasa. Uhlsport kupitia Romario imeshinda tenda hiyo baada ya kushindwanishwa na makampuni mengine matatu. Magori ametoa raia kwa wanachama na wapenzi wa Simba kunua jezi halisi zitakazosambazwa na kampuni hiyo nchini kote kuanzia leo. Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa Romario Sport Minhaal Dewji alisema jezi walizotengeneza zina ubora kama zile za timu ya Taifa na wanazikaribisha timu zingine ili kupata huduma hiyo.
4
Lulu aliye nje kwa dhamana atapanda kizimbani mahakamani hapo baada ya kusomewa maelezo ya awali karibu miaka miwili na nusu iliyopita. Msanii huyo anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kumuua Kanumba bila kukusudia kinyume cha Kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu.Inadaiwa Lulu alimuua Kanumba bila ya kukusudia Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu huyo Sinza Vatican, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya kesi za mauaji ya bila kukusudia iliyotolewa na Mahakama Kuu Dar es Salaam jana, kesi hiyo itasikilizwa siku hizo na Jaji Sam Rumanyika. Kesi hiyo inaanza kusikilizwa baada ya kupangiwa Jaji kufuatia upelelezi kukamilika.Mara ya kwanza Lulu alipandishwa kizimbani Aprili 11, 2012 mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es Salaam wakati huo, Augustina Mbando ambapo alisomewa mashitaka ya mauaji.Hata hivyo, Februari 18, 2014 akisomewa maelezo ya awali Lulu alikiri mahakamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kanumba na pia kusema kulikuwepo ugomvi baina yao siku ya tukio la kifo cha mwigizaji huyo.Lulu aliachiwa kwa dhamana Januari 29, 2013 baada ya kesi hiyo kubadilishwa hati ya mashitaka kutoka kwenye kesi ya mauaji kwenda mauaji ya bila kukusudia ambapo badiliko hilo lilimpa nafasi ya kupata dhamana.Katika kesi ya msingi namba 125 ya mwaka 2012, inadaiwa Aprili 7, 2012 Sinza Vatican Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia. Lulu alipelekwa rumande gereza la Segerea hadi mashitaka yalipobadilishwa akapata dhamana.
4
SERIKALI imeitaka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kufanya utafi ti wa taasisi za kifedha hasa taasisi ndogo nchini kuona kama kweli riba wanazotoa kwa wateja wao zina sababu ya msingi au zinatolewa kwa riba kubwa kwa kujilimbikizia faida kubwa na kuwaumiza wateja, wakiwemo wajasiriamali na watumishi hasa wa kada ya chini.Rai hiyo imetolewa jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, wakati akifungua hafla ya kugawa hati za viwanja kwa wanachama wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo- Hazina Saccos.Dk Mpango alizitaka benki na taasisi ndogo za fedha nchini kuangalia upya namna ya ukokotoaji wa riba kwa kuwa zinawaumiza wananchi wakiwemo wajasiriamali na watumishi wanaozitegemea katika kupata mitaji yao.“Kuna taasisi moja ambayo inakopesha fedha kwa watumishi wa serikali wakiwamo walimu, kwa riba ya asilimia 32 ilihali wao wanachukua mikopo benki kwa asilimia 20 ni hatari kweli, asilimia 32 ni riba kubwa mno,” alisisitiza. Alisema mchango wa Saccos unatambulika kama nyenzo muhimu ya kupunguza umasikini, ndio maana serikali imetunga Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha kuzisimamia taasisi ndogo za fedha ili kuwapunguzia adha wafanyakazi na wajasiriamali wanaokopa fedha katika taasisi hizo kwa riba kubwa na masharti ya kinyonyaji.Aliwasihi viongozi wa Saccos zote nchini kufanya kazi kwa bidii, uadilifu, weledi na kutumia maarifa ili kufanikisha ndoto za wanachama wao kwa kuwa Saccos ndio kimbilio kwa watumishi wengi hasa wa kada za chini. Alisema kuna changamoto ya ubadhirifu katika Saccos nyingi nchini, jambo ambalo asingependa kulisikia kwa Hazina Saccos ambayo yeye ni mwanachama, hivyo ameitaka pamoja na nyingine kuweka mifumo imara itakayowezesha kutambua upotevu wa mali zao ili kudhibiti mapema kabla ya madhara makubwa kujitokeza.
3
Kampuni ya Saruji ya Dangote Tanzania imedhamiria kukabiliana na uhaba huo ikipanga kuzalisha zaidi ya tani 6,000 kwa siku kutoka chini ya tani 3,000 za sasa.Kampuni hiyo imesaini mkataba wa kuuziwa gesi asilia kwa miaka 20. Kampuni hiyo inayomilikiwa na bilionea namba moja Afrika, Aliko Dangote wa Nigeria na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).Kabla ya ahadi hiyo itakayoanza kutekelezwa katika miezi ya hivi karibuni, Dangote ilikuwa inatumia nishati ya dizeli kiasi cha lita 160,000 kwa siku ili kuzalisha tani 2,000 hadi 2,500 kwa siku, hivyo kugeuka mzigo mkubwa katika uzalishaji.Hata hivyo, ili kupunguza tatizo la uhaba wa saruji lililojitokeza hivi karibuni, kampuni hiyo iliongeza uzalishaji na kufikia tani 3,300 badala ya zile za siku zote tani 2,000.Utiaji saini mkataba wa mauziano ya gesi asilia yalifanyika Dar es Salaam jana baina ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha Dangote Tanzania, Jagat Singh Rathee na Kaimu Mkurugenzi wa TPDC, Kapulya Musomba.Kwa kuanzia, TPDC itaiuzia Dangote gesi ya ujazo wa futi milioni nane. Rathee amesema tatizo kubwa lililokuwa likikabili uzalishaji wa saruji kwa kiwanda hicho ni gharama kubwa za uzalishaji kwa kutumia umeme unaotokana na nishati ya dizeli.Amesema uzalishaji saruji kutokana na nishati ya gesi utaanza ndani ya siku 45 na kwamba sasa wanamalizia ujenzi wa kuingiza gesi hiyo na kuzalisha megawati 35 za umeme kwa kuanzia na baadaye kufikia megawati 45 za umeme zitakazosaidia kuzalisha saruji kwa bei nafuu.Alisema katika upatikanaji wa gesi asilia itasaidia katika uzalishaji wa uhakika, utunzaji wa mazingira, kuhakikisha msaada huo unakuwa na manufaa kwa Tanzania na kampuni hiyo yenye makao yake makuu nchini Nigeria.Musomba alisema matumizi ya gesi asilia katika kiwanda hicho ni katika awamu mbili ile ya kuzalisha umeme ambapo miundombinu iko tayari na awamu ya pili kuchoma udongo na tayari imekamilika.Amesema katika kukamilisha Tanzania ya viwanda, wanatimiza wajibu wao kwa wakati na kufuata taratibu za nchi mpaka sasa Dangote kinakuwa kiwanda cha 42 kuzalisha kwa kutumia gesi asilia huku katika mwaka huu wa fedha wakitarajia kuongeza viwanda vingine saba.Musomba amesema katika mkataba huo wa miaka 20 kwa kuwauzia gesi ya ujazo wa futi za ujazo milioni nane kwa awamu ya kwanza huku awamu ya pili ikizidi futi za ujazo milioni ishirini huku bei ya kuuziana itapangwa na mdhibiti, Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Umeme (EWURA).Amesema mpaka sasa kabla ya kuingizwa kwa Dangote viwanda vinavyotumia gesi asilia vilikuwa vikitumia gesi asilia za futi za ujazo milioni 15 mpaka milioni 17 na Dangote itaongeza matumizi ya viwandani na kufikia futi za ujazo milioni 23 na baada ya ya miaka miwili viwanda vyote vitakuwa vikitumia futi za ujazo milioni 40.Amesema nchini gesi asilia imeanza kutumika mwaka 2004, lakini viwanda vimeanza kutumia gesi katika mwaka wa fedha 2006/07 kwa ushirikiano na kampuni ya Pan-African, lakini sasa uunganishaji gesi viwandani unafanywa na TPDC wenyewe.Amesema kiwanda cha Dangote ni cha pili kikitanguliwa na kile cha Goodwill cha Mkuranga, ndivyo vilikuwa vikiendeshwa na TPDC wenyewe.Hivi karibuni uhaba wa saruji uliingia Tanzania na kusababisha bei kupaa mpaka Sh 24,000 kwa mfuko, jambo lililomlazimu Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya kufanya mkutano na wazalishaji, wasambazaji, wasafirishaji wa saruji na kampuni zinazozalisha makaa ya mawe.Manyanya aliwapa mwongozo wazalishaji hao kwa kuanza kuelezea kiwango cha saruji walichokuwa wakizalisha kwenye uzalishaji wa kawaida na kisha kuelezea kiwango ambacho ndani ya wiki hii wamekuwa wakizalisha.Baadhi ya wawakilishi wa viwanda hicho walieleza changamoto wanazokabiliana nazo, akiwemo Meneja Mkuu wa Twiga Cement, Alfonso Velez ambaye alifafanua kuwa kiwango cha uzalishaji kilishuka kutokana na kuzima mitambo ya mwezi uliopita kwa ajili ya matengenezo lakini kwa sasa uzalishaji umerejea kama kawaida.Mwakilishi wa Tanga Cement, Benedict Lema ambaye alikiri kushuka kwa kiwango cha uzalishaji kwenye kiwanda chake, alisema katika uzalishaji wa kawaida kiwanda kinaweza kuzalisha 3,500 hadi 4,000 kwa siku na hutumia tani 600 za makaa ya mawe kuendesha mtambo wa kuzalisha kiasi hicho cha saruji.Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji kutoka Shirika la Madini ya Taifa (Stamico), Alex Rutagwelela alibainisha ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa makaa ya mawe, mwezi ujao itaanza kuzalisha tani 18,000 katika Kijiji cha Kaburo wilayani Ileje.Mwaka jana, Waziri wa viwanda na Biashara, Charles Mwijage alisema viwanda vya saruji nchini vinatarajiwa kuongeza uzalishaji maradufu kutoka tani milioni 10.8 za wakati huo hadi kufikia tani milioni 20 kwa mwaka.Alisema kuna viwanda vya saruji takribani 11 ambavyo vina uwezo wa kuzalisha tani milioni 10.8 wakati mahitaji halisi yaa nchini pekee ni tani milioni 4.7 kwa mwaka.Anasema kuongezeka kwa uwezo wa uzalishaji wa tani za ziada umelenga katika kuhakikisha wanayateka masoko yaliyoko katika nchi za Afrika Mashariki, Afrika yote na hata nje ya Afrika, hasa nchi za Uarabuni.
3
Mkurugenzi Mkuu wa Fastjet nchini, Nico Bezuidenhout amesema mwishoni mwa wiki kuwa, makubaliano hayo yatakuza biashara ya Fastjet kwa kutanua wigo wa kuuza tiketi duniani.Amesema wateja wataweza kufanya maandalizi ya safari, kununua tiketi na kuona mfumo wa safari za Fastjet kirahisi na kutumia huduma zao."Kwa kuwa hata IATA imesema Fastjet itakuza biashara yake kwa asilimia 8 kwa mwaka huu, makubaliano haya na Travelport yataiunganisha Fastjet na mawakala wa safari za anga zaidi ya 68,000 hivyo kwetu ni fursa kubwa ya kukuza biashara," alisema Bezuidenhout alipozungumza na waandishi wa habari.Makamu wa Rais wa Travelport kwa Bara la Ulaya, nchi za Kiarabu na Afrika, Philip Saunders, alisema teknolojia ambayo kampuni yake inatumia itaiongezea mauzo Fastjet kwa kuwa itafahamika kwa mawakala zaidi duniani.Saunders alisema wanatarajia kufanya kazi bega kwa bega na Fastjet katika kufanikisha malengo yake na wakati huo huo kuifanya Travelport kuendelea kuwa kiongozi kwenye sekta ya ukataji tiketi za usafiri wa anga Afrika.
5
Na Kulwa Mzee-Dar es Salaam MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemwonya na kumwambia Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), kwamba kadi za onyo kwa ajili yake zimeisha kutokana na kushindwa kuhudhuria mahakamani siku ya kesi. Kauli hiyo ilitolewa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya kubaini kwamba ilitolewa hati ya kumkamata mbunge huyo kwa kushindwa kufika mahakamani. Halima Mdee alipotakiwa kujitetea aliinuka na kujieleza kuwa amefika mahakamani hapo akiwa na nyaraka za safari ikiwamo tiketi na VISA na kwamba taarifa za safari alimpa wakili. Kwa upande wa wakili wao, Hekima Mwesiga aliieleza mahakama kuwa nyaraka za kuiarifu mahakama juu ya safari ya Halima Mdee nje ya nchi kwa bahati mbaya hakuziwasilisha, alikuwa nazo Peter Kibatala ambaye alikuwa akiendesha kesi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu. “Tutaonana wabaya katika hili ni lazima unapofanya kitu adabu yake ifuatwe, Wakili hakufuata taratibu na Halima kabla ya kusafiri ulipaswa kutoa taarifa mahakamani ili uweze kupata ruhusa ya mahakama lakini haukufanya hivyo. “Sasa nafikiri wote tufuate taratibu za kuhudhuria mahakamani, Halima Mdee kadi zako  za kukuonya zimeisha tafadhali,”alisema Hakimu. Mdee na wabunge wengine wa Chadema, Mwita  Waitara, Saed Kubenea  na makada wao wanatuhumiwa kumjeruhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresa Mmbando.  Kabla ya onyo hilo, mahakama ilisikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka uliotolewa na Mrakibu wa Polisi, ambaye pia ni Msaidizi wa Operesheni Ilala, Eugen Mwampondele. Mwampondele alidai siku ya tukio alimwona Rafii Juma na Halima Mdee wakimkunja Theresa Mmbando ili awape nyaraka. Shahidi huyo alidai waliompiga Mmbando hawapo mahakamani. Washtakiwa katika kesi hiyo ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea, Diwani wa Kata ya Kimanga, Manase Njema (56), Halima Mdee (37) na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (40). Wengine ni mfanyabiashara na kada wa chama hicho, Rafii Juma (21)pamoja na Diwani wa Kata ya Saranga, Ephreim Kinyafu (33). Inadiwa kuwa Februari 27, 2016 katika Ukumbi wa Karimjee Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam watu hao walimjeruhi Theresia na kumsababishia majeraha mwilini wakati wa uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam.
3
Na ASHA BANI -DAR ES SALAAM CHAMA cha Wananchi (CUF) upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, leo wanatarajia kuzindua jengo jipya la ofisi lililopo eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam. Taarifa za ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa ofisi hizo zitatumiwa na viongozi wakiwemo wabunge wanaomuunga mkono Maalim Seif. Akithibitisha taarifa hizo, Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, Mbarara Maharagande, alisema uzinduzi wa ofisi hiyo mpya utafanyika wakati wowote kuanzia sasa. Hatua ya kuzindua jengo hilo imekuja wakati ambapo chama hicho kikiwa katika mgogoro mkubwa wa uongozi uliotokana na uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, kumrudisha katika nafasi yake ya uenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba na kisha kutwaa jengo lenye ofisi za chama hicho lililopo Buguruni jijini Dar es Salaam. “Tutazindua jengo jipya iwe leo au kesho au muda wowote kuanzia sasa, lakini ni jengo la wabunge wote kufanyia shughuli zao hapo na kupanga mikakati mbalimbali ya kukitangaza na kukiimarisha chama,” alisema Maharagande. Wakati Maharagande akisema hayo, taarifa ambazo gazeti hili limezipata toka kwa vyanzo vyake ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa jengo hilo pia litakuwa na ofisi ambazo zitatumiwa na viongozi wa CUF akiwemo Maalim Seif mwenyewe. Kwa muda wa miezi sita sasa pande mbili za uongozi zimekuwa zikilumbana juu ya uhalali wa maamuzi ya Mkutano Mkuu wa Taifa wa chama hicho uliofanyika Agosti mwaka jana ambao pamoja na mambo mengine ulilenga kumwondoa Profesa Lipumba. Hatua hiyo ilizua tafrani na hata wajumbe kurushiana masumbwi ndani ya ukumbi hali iliyosababisha kuvunjika kwa mkutano huo. Siku chache baadaye Baraza Kuu la uongozi lilikutana na kutangaza kumvua uanachama wa CUF Profesa Lipumba jambo ambalo lilipingwa na Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Mutungi ambaye alisema taratibu za kufukuzwa kwa Mwenyekiti huyo hazikufuatwa. Mapema wiki hii upande wa uongozi wa CUF, chini ya Mwenyekiti anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Lipumba, ulidaiwa kulamba Sh milioni 369.378 za ruzuku kinyume na utaratibu. Ilielezwa kuwa fedha hizo zilitolewa ndani ya siku moja katika matawi matatu tofauti ya Benki ya NMB kwa kutumia akaunti ya chama na baadaye kuhamishiwa kwa mtu binafsi. Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF ambaye hatambuliwi na Msajili, Julius Mtatiro, alisema fedha hizo zilitolewa kutoka Hazina na kupelekwa NMB tawi la Temeke. Wakati Mtatiro akidai hayo, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa CUF, Abdul Kambaya, ambaye yupo upande wa Lipumba, alidai fedha hizo zimetolewa kihalali kama walivyofanya upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad ambao nao walitoa Sh milioni 80 kupitia Benki ya NBC. Pamoja na hali hiyo, Mtatiro alisema fedha hizo ziliingizwa katika akaunti binafsi ya mtu aliyetambulika katika muamala kwa jina la Mhina Masoud Omary. Alisema kwa niaba ya Baraza Kuu la Uongozi la CUF ambalo limemteua yeye kuongoza, hana budi kuwajulisha wanachama kuwa CUF imeibiwa fedha hizo za ruzuku ambazo alidai zimetoroshwa na watu wasiojulikana.
3
SERIKALI imesitisha safari za ndege kwenda nchini Afrika Kusini mpaka wajiridhishe kwa maandishi kuhusu usalama wa abiria na ndege kutokana na vurugu zinaozendelea nchini humo.Aidha, serikali imetangaza kuwa mwezi Novemba wataingiza nchini ndege mbili aina ya Bombardier na Dreamliner huku wakikamilisha manunuzi ya ndege mpya mbili aina ya Airbus.Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amebainisha hayo wakati akizindua rasmi Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuwa mamlaka kisheria kutoka kuwa wakala na kubainisha kuwa baada ya ndege ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) iliyokuwa ikishikiliwa Afrika Kusini kuwasili juzi jioni Dar es Salaam.Kamwelwe alisema ndege hiyo kwa mujibu wa ratiba ilitakiwa leo kufanya safari yake Afrika Kusini, lakini wamesitisha kutokana na fujo zinazofanywa na vijana hivyo hawawezi kupeleka abiria na chombo hicho kwani hawaamini usalama wao.“Tutasitisha kwa muda mpaka tutakapopata mawasiliano ya maandishi kutoka Serikali ya Afrika Kusini kuhusu usalama wa abiria na chombo chetu,” alisema waziri huyo.Alisema wanafanya utaratibu kuhakikisha abiria watapelekwa kupitia ATCL kwa kutumia ndege nyingine kwa lengo la kulinda safari za ndege hiyo kwenda Afrika Kusini ili isipotee.Amesema baada ya kurejea kwa ndege hiyo iliyokuwa ikishikiliwa imefanyiwa uchunguzi kwani ilikaa kwa siku zaidi ya nane na imebainika haina matatizo itaendelea na ratiba ya safari zake kama kawaida.Alisema kutokana na changamoto hiyo, kulitokea kuathirika kwa safari kwa baadhi ya maeneo, lakini sasa zimekaa sawa wakati serikali ikijiandaa kupokea ndege mpya Novemba mwaka huu.Akizungumzia sakata la kukamatwa kwa ndege na maamuzi ya serikali, alibainisha kuwa baada ya hukumu kutolewa na ndege kurejea nchini wanasheia wanaendelea kushughulikia hukumu iliyotolewa ili aliyeshtaki anatakiwa kulipa gharama na wataendelea kutoa taarifa.
5
Na Hadija Omary, Lindi Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Kanda ya Mtwara imezipatia vifaa tiba vyenye thamani ya Sh milioni 33.3 halmashauri mbili za mkoa wa Lindi kwa lengo la kuboresha huduma mbalimbali za afya kwa wananchi wake. Vifaa hivyo ni pamoja na vitanda vinane kwa ajili ya kujifungulia na darubini sita zikazofanya kazi za kiuchunguzi wa kimaabara katika vituo mbalimbali vya afya. Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo kwa uongozi wa halmashauri hizo, Meneja wa Bandari mkoani Mtwara Nelson Mlali amesema lengo la kutoa msaada huo ni kuboresha huduma za Afya kwa wananchi. “Sisi tunaanza tu, lakini wenzetu wengi wanatusikia, nina imani watajitokeza kutuunga mkono ili kutatua changamoto hizi za afya kwani ni wazi kwamba changamoto za sekta ya afya ni nyingi na hatutaweza kuzimaliza kwa siku moja au kumaliza kwa kujitolea kwa taasisi nyingine hivyo natoa wito kwa taasisi nyingine kuunga mkono jitihada hizi,” amesema Mlali. Meya wa Manispaa ya Lindi, Mohamed Lihumbo ameishukuru mamlaka hiyo kuwa msaada huo na kuongeza kuwa umefika kipindi muafaka wakati ujenzi wa vituo vipya vya afya ukiendelea kwenye kata mbalimbali. Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Dk. Ally Zuberi na Mganga Kituo cha Afya cha Mjini cha Manispaa Lindi, Richard Juma wamesema upatikanaji wa vifaa hivyo utawasaidia kutekeleza majukumu ya utoaji bora wa huduma kwa wagonjwa wanaofika kupata tiba.
3
WADAU wa mawasiliano wameshitukia athari zitakazowapata endapo serikali itazingatia msimamo wake wa kusitisha laini zisizo na usajili wa alama za vidole, kwa kuamua kukutana kuweka mikakati ya pamoja kuhimiza wananchi kusajili.Zikiwa zimebaki siku 24 kabla ya ukomo wa usajili wa laini za simu, Mwenyekiti wa Kamati ya Uhamasishaji kuhusu usajili wa laini, Jackson Mmbando alisema jana kwamba leo wanafanya mkutano jijini Dar es Salaam utakaohusisha zaidi ya wadau 250.Mkutano huo wa pamoja utahusisha taasisi mbalimbali zikiwamo benki, watoa huduma, wasanii na watu maarufu ambao kufungwa kwa laini za simu kutawaathiri kimapato na mawasiliano.“Lengo ni kuwashirikisha kuhusu athari zitakazotokea endapo serikali itasimamia msimamo wake wa kufunga laini zote ambazo hazijasajiliwa. Tunataka wadau wafahamu kwamba wao pia wanapaswa kuzungumza kuwaambia wateja na mashabiki umuhimu wa kusajili,” amesema Mmbando.Kamati hiyo maalumu iliundwa hivi karibuni na kampuni zote za simu za mkononi chini ya uratibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), lengo likiwa kuhamasisha na kuelimisha umma kuhusu usajili wa laini kabla ya Desemba 31, mwaka huu.Baada ya kubaini takribani mikoa 14 ambayo haijafanya vizuri katika usajili wa laini, Mmbando alisema wamewaomba wakuu wa mikoa husika wawatangazie wananchi wajitokeze kusajili kabla ya muda wa ukomo.Miongoni mwake ni Mjini Magharibi, Shinyanga, Singida, Mara, Kilimanjaro, Manyara, Lindi, Mtwara, Ruvuma na Tabora.Akizungumzia sababu, alisema, “kuna wengine ukiwapigia wanakuambia kuwa hawana muda. Unakuta kuna watu wanazo namba za NIDA lakini hawajaenda kusajili wanasubiri dakika za mwisho.” Mikakati mingine ni kuwezesha vitambulisho vya taifa hadi ngazi ya mitaa.
3
KANO, NIGERIA MSHAMBULIAJI wa klabu ya Leicester City na timu ya Taifa ya Nigeria, Ahmed Musa, amefanikiwa kufungua kituo cha pili cha mafuta mjini Kano nchini humo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, amewafurahisha idadi kubwa ya mashabiki wa soka nchini humo kwa kuongeza kituo cha pili cha mafuta ambacho kinaweza kutoa huduma kwa gari sita kwa wakati mmoja. Kituo hicho kipo umbali wa kilomita 500 kutoka kwenye mji aliozaliwa, lakini ameamua kukiweka umbali huo ili kuweza kuwahudumia mashabiki wake wengine ambao wapo mbali na eneo lake. Maisha ya wachezaji wa soka si ya miaka mingi sana, hivyo mchezaji huyo ameamua kutumia fedha zake vizuri kwa kuwekeza katika biashara mbalimbali ikiwa pamoja na kituo kikubwa cha mazoezi. Mchezaji huyo alikuwa nchini humo hivi karibuni wakati wa michezo ya kimataifa ya kalenda ya Fifa, lakini aliweza kutumia nafasi hiyo kufungua kituo hicho na kuna wakati alikuwa anatoa huduma ya mafuta yeye mwenyewe. Kitendo hicho cha kutoa huduma yeye mwenyewe kiliwafanya mashabiki mbalimbali kujitokeza na magari yao ili awahudumie na kisha kupiga naye picha. Kupitia ukurasa waka wa Instagram, mchezaji huyo aliweza kuposti baadhi ya picha huku akiwa anatoa huduma na nyingine akiwa na mashabiki wake. Mchezaji huyo alijiunga na klabu ya Leicester City mwaka jana baada ya kufanya vizuri kwenye klabu yake ya CSKA Moscow ya nchini Urusi huku akifunga mabao 42 kutokana na michezo 125 na tangu amejiunga na Leicester City amefanikiwa kucheza michezo 18 ya ligi na kupachika mabao 2, wakati huo katika timu ya Taifa akicheza jumla ya michezo 63 na kupachika mabao 13.
4
MRADI mpya wa kushughulikia taka za afya hospitalini, unaotumia kondo la nyuma la mama baada ya kujifungua kuzalisha gesi, umeonesha mafanikio makubwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala.Akizungumzia mafanikio ya miaka minne ya hospitali hiyo katika awamu ya tano, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala, Dar es Salaam, Dk Daniel Mkungu alisema mradi huo umeonesha mafanikio makubwa hospitalini hapo na tayari hospitali ya Sinza nao wanaanza kuutekeleza.“Wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto, kwa kushirikiana na Shirika na Maendeleo ya UNDP, walibuni mradi huu na sisi tukaupokea na kuutekeleza na ni miaka miwili tangu tuwe nao tumeona mafanikio, alisema Dk Mkungu ambaye pia ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya akinamama.Akiuzungumzia utekelezaji wa mradi huo, Dk Mkungu alisema baada ya wizara kuuibua hospitali hiyo iliutekeleza ikiwa ni mradi wa majaribio kwa kujengwa mtambo wa kuchakata na kusindika makondo hayo pamoja na mabaki ya vyakula kisha kuzalisha gesi ambayo hutumika kwa matumizi mbalimbali hospitalini hapo.Dk Mkungu alisema gesi inayozalishwa ni aina ya Methane ambayo huunguzwa na kutumika kuchemshia maji kwenye wodi ya wazazi waliojifungua hospitalini hapo na hivyo kuondoa adha ya awali ya ndugu wa mzazi aliyejifungua kuleta maji ya moto kutoka nyumbani.“Tumefurahi kwa mtambo huu kujengwa na kuwa na mafanikio chanya, leo hakuna tena harufu mbaya ya taka zinazozalishwa hospitalini hapa kama makondo ya nyuma, na mabaki ya vyakula nao yanaingia kwenye mtambo huo na kuchakatwa kisha kusindikwa na kuzalisha nishati hiyo ya gesi,”alisema Dk Mkungu.Alisema mtambo huo umezuia harufu mbaya iliyokuwa inatoka hospitalini hapo ya taka na makondo hayo na kwamba hivi sasa kondo la nyuma limegeuka kuwa bidhaa na kwamba kwa siku zijazo watasambaza gesi hiyo kwenye jiko la kanteni hospitalini hapo ili itumike kupikia.”Hospitali nyingine zinaweza kutumia fursa hii kuzalisha gesi na hivyo kulinda mazingira na kuokoa gharama za nishati kwenye matumizi mbalimbali , kama kupikia na wakati huo huo kulinda mazingira,”alisema Dk Mkungu.Akizungumzia hali ya mazingira kwa sasa hospitalini hapo, Ofisa afya wa hospitali hiyo, Sifa Mgaya alisema mazingira ni bora na hakuna harufu mbaya tena inayotoka ya taka hospitalini hapo.“Mtambo huu umekuwa mkombozi kwetu umesaidia kuondoa harufu kwa sababu kondo la nyuma asilimia 80 ni maji kuliteketeza huchukua muda mrefu na hata ukichoma bado kuna moshi unaoenda angani, lakini sasa tumegeuza taka hizi kuwa malighafi,”alisema Mgaya.Alisema mtambo huo unazalisha gesi kiwango cha kubiki mita 2.5 na kwamba kwa siku huzalisha wanawake kati ya 20 hadi 100 kutofautiana na msimu kwani kuna msimu huzalisha hadi mama 100 kwa siku.Mgaya alisema teknolojia hiyo ya ujenzi wa mtambo kama huo barani Afrika umeanza kutekelezwa kwenye nchi nne ambazo ni Ghana, Mauritus, Zambia na Tanzania.Nchini Tanzania mradi huo wa majaribio unatekelezwa kwenye hospitali na vituo vya afya vitano ambavyo ni hospitali hiyo ya Mwanyamala, Sinza, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Hospitali ya Mbagala Rangi tatu na kituo cha afya cha Buguruni cha Anglikani.Alisema gharama za ujenzi wa mtambo huo ni kati ya shilingi milioni 15 hadi 25 kulingana na mazingira ya eneo.
3
IMEBAINIKA kuwa wasomi wa kiwango cha elimu ya shahada ya uzamivu ni muhimu si tu katika taasisi za kitaaluma bali pia katika taasisi nyingine za kimaendeleo kutokana na uwezo walionao katika kusaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali.Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Masomo ya Juu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) Profesa Hosea Rwegoshora wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa wanafunzi wa Shahada za Utafiti za Uzamili na Uzamivu kwa mwaka wa masomo wa 2019/20 iliyofanyika Kinondoni, Dar es salaam.Alisema kuna uhusiano mkubwa kati ya utafiti, matokeo ya utafiti na ubunifu katika utatuzi wa changamoto zinazoikabili jamii kitu ambacho ni moja ya kazi zitokanazo na watafiti katika mchakato wa kusoma.“Kuna shahada za uzamivu ambazo zimejikita katika mlengo wa kutatua changamoto za jamii hivyo kuleta ubunifu ndani yake”, alisema Profesa Rwegoshora.Hata hivyo, alisema kwa uzoefu wake baadhi ya wanfunzi wanaofanya tafiti katika ngazi ya shahada za uzamili na uzamivu hutoa mapendekezo ambayo hayatekelezeki kitu ambacho hakikutakiwa.Mkurugenzi Msaidizi wa Kurugenzi ya Masomo ya Juu, Daktari Jacob Lisakafu amesema kama chuo wameamua kuwapa wanafunzi mafunzo hayo ikiwa ni njia ya kutekeleza kwa vitendo nia ya chuo kufanikisha usomaji wao kuwa rahisi hususani katika masuala ya tafiti na mifumo ya chuo hicho.Mkurugenzi wa Kituo cha Mkoa cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania cha Kinondoni Daktari Hyasinta Kessy aliwakaribisha wanafunzi hao katika chuo hicho na kuwashauri umuhimu wa umakini katika masomo yao ili waweze kuhitimu kwa muda muafaka ili wasaidie jamii.“Kwa kuwa masomo ya shahada ya uzamili na uzamivu yanaongozwa kwa ushirikiano kati ya msimamizi wa utafiti na mwanafunzi nawaasa kuwajibika, kujituma na kuheshimu wasimamizi wenu,” alisema Dk Kessy.Hata hivyo kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wanafunzi wanaofanya shahada za uzamili na uzamivu kutokana na mifumo ya usimamizi katika taasisi nyingi za elimu ya juu nchini.
3
MBUNGE wa Geita Mjini (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantine Kanyasu amewataka wakulima wa zao la pamba kuwa wavumilivu badala ya kuuza pamba yao kwa walanguzi kwa bei ya chini huku serikali ikiendelea kuwatafutia soko zuri.Amesema serikali imeahidi kuwa kama pamba hiyo haitanunuliwa kwa bei elekezi ya kilo moja kwa Sh 800 hadi Agosti, mwaka huu itainunua ili kuwasaidia. Hatua hiyo ya serikali imekuja baada ya wafanyabiashara wengi kushindwa kununua kwa bei hiyo kutokana bei ya soko la pamba duniani kuporoka. Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika katika eneo la Kasamwa mkoani Geita juzi, Kanyasu alisema wafanyabiashara wameshindwa kukopa fedha benki kwa ajili ya kununua pamba hiyo kutokana na kukosekana kwa soko la kuiuza.Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya wakulima wamekuwa wakiuza pamba hiyo kwa Sh 500 kwa kilo moja kwa walanguzi hali inayowadidimiza kiuchumi. Kanyasu alitaja hatua ambazo serikali inachukuwa kuwatafutia soko wakulima hao kuwa ni kuzungumza na serikali ya Vietnam ambayo imeonesha kuwa tayari kununua pamba hiyo kwa wakulima.Aidha, aliwaeleza wakulima hao kuwa waziri wa kilimo anapanga kutembelea mkoa huo kwa ajili ya kuzungumza nao. Naye Juma Kaludushi ambaye ni mkulima wa zao la pamba alisema wakulima wengi akiwamo na yeye wamekuwa wakiuza pamba yao kwa walanguzi kwa bei ya chini kwa hofu kuwa itaharibikia mikononi mwao. “Pamba ipo majumbani mwetu muda unakwenda bora tuuze tu kwa walanguzi ili isiharibike kuliko kupata hasara kabisa,” alisema.Mkulima mwingine, Ester Nalamo, alisema amelazimika kuuza pamba kwa bei ya chini ili aweze kuwalipia ada watoto wake kwa kuwa hana chanzo kingine cha mapato zaidi ya zao hilo.
3
WASHINGTON, MAREKANI ALIYEKUWA Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden, amejiunga rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais kupitia kwenye chama chake cha Democratic, huku akirusha kombora kuwa Marekani itakuwa hatarini iwapo Rais Donald Trump atashinda tena kwenye uchaguzi ujao. Katika video iliyotumwa kwenye ukurasa wa Twitter, Biden amesema Marekani imo kwenye mapambano ya kuenzi misingi ya taifa hilo na hatakubali kuendelea kutazama ikivurugwa na utawala wa Trump. Biden mwenye umri wa miaka 76, ni miongoni mwa wagombea wenye nafasi nzuri ya kupitishwa ndani ya chama hicho pamoja na Seneta Bernie Sanders wa Jimbo la Vermont ambaye anaongoza kwenye kura za maoni. Biden lazima atachuana na wagombea wengine wapatao 20 ndani ya chama chake ambao wanawania kumkabili Trump katika uchaguzi wa mwaka 2020. Kwa upande wake, Rais Donald Trump amemrushia kijembe Joe Biden kwa kusema kuwa ni mtu mwenye kulala sana. Akiandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, amesema: “Joe Biden mwenye usingizi mwingi, karibu kwenye mchuano.” Hata hivyo, Trump ameonyesha wasiwasi wake kutokana na uwezekano wa Biden kuibuka mshindi kwenye uteuzi wa mapema wa ndani ya Chama cha Democrat kutokana na uelewa alionao makamu huyo wa zamani wa Rais wa Marekani.
2
MKUTANO Mkuu maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, umemchagua kwa kura nyingi mkuu wa wilaya hiyo, Miraji Mtaturu kugombea nafasi ya ubunge Jimbo la Singida Mashariki kwenye uchaguzi mdogo utakaofanyika Julai 31, mwaka huu.Katibu Sekretarieti CCM Taifa, Salum Hatibu Reja, ambaye alikuwa msimamizi wa mkutano huo amesema DC Mtaturu amejizolea jumla ya kura 396 kati ya 600 zilizopigwa na wajumbe.Katika mkutano huo, mwanachama Thomas Kitima alifuatia kwa kupata kura 79, Chiku Gallawa (40) wakati wagombea wengine 10 waliambulia kati ya kura moja na 17.Mara baada ya kutangazwa kwa kinyang’anyiro cha kuwania jimbo hilo katika uchaguzi mdogo, takribani wanachama wa CCM 13 walijitokeza kuomba kuteuliwa kupeperusha bendera ya Chama kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) hivi karibuni ilitangaza Uchaguzi Mdogo katika Jimbo la Singida Mashariki mkoani hapa utakaofanyika Julai 31, mwaka huu.Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Semistocles Kaijage amesema, amefanya hivyo kutokana na barua ya Spika wa Bunge, Job Ndugai inayoeleza kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Tundu Lissu amepoteza sifa baada ya kushindwa kuwasilisha kwake tamko la mali na madeni pamoja na kushindwa kuhudhuria mikutano saba mfululizo bila ruhusa ya Spika.Jimbo la Singida Mashariki limekuwa chini ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambapo Lissu amekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa vipindi viwili kuanzia mwaka 2010.
3
NA ZAINAB IDDY, DAR ES SALAAM MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini anayetamba na wimbo wake wa Mdogomdogo, Nasseb Abdul ‘Diamond Platinumz’,  juzi ametwaa tuzo mbili katika tuzo za Afrika Music Magazine Award ‘AFRIMMA 2014’ kupitia kipengele cha mwanamuziki bora wa kiume Afrika Mashariki zilizofanyika Eisemann Center Richardson, Texas, Marekani. Mkali huyo wa wimbo wa My Number One, alishinda tuzo hizo ikiwemo ya Msanii bora wa Afrika Mashariki na ile ya Wimbo bora wa kushirikiana aliofanya na msanii Davido wa Nigeria. Katika tuzo ya Msanii bora wa kiume wa Afrika Mashariki, Diamond aliwashinda Ben Pol wa Tanzania, Bebe Cool wa Uganda, Wyre wa Kenya, Jackie Gosee wa Ethiopia na Navio wa Uganda. Diamond aliibuka kidedea katika Wimbo bora wa kushirikiana akiwabwaga  T Pain na 2 Face – rainbow, Khona ya Uhuru na Mafikizolo wa Afrika Kusini, Surulere remix ya Dr Sid wa Nigeria, Amani aliyewashirikisha Waganda Radio na Weasel ‘Kiboko changu’, J Martins akimshirikisha Dj Arafat ‘Touching body’ na Rebees na Wizkid ‘Slow down’. Katika tuzo hizo pia msanii mwingine wa Tanzania, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ alitwaa tuzo ya Msanii bora wa kike Afrika Mashariki aliyewabwaga Aster Aweke wa Ethiopia, Rema wa Uganda, Avril wa Kenya, Victoria Kimani wa Kenya na Irene Ntale wa Uganda. Naye Mtanzania Sheddy Clever alinyakua tuzo ya Prodyuza bora baada ya kuwashinda Don Jazzy wa Nigeria, Dj Oskido wa Afrika Kusini, Shizz wa Nigeria, Killbeatz wa Ghana, Oskido wa Afrika Kusini, Nash Wonder wa Uganda na Ogopa wa Kenya. Tuzo ya Mtayarishaji bora wa video ilinyakuliwa na Ogopa Dj’s ambao ndio waliofanya video ya ‘My number One′ ya Diamond Platnumz. Diamond akizungumzia ushindi huo kupitia ukurasa wake wa Instagram, alimshukuru Mungu kwa kumwezesha kupata tuzo hizo. “Kwanza ya yote napenda nimshukuru sana Mwenyezi Mungu, mama, familia, na Management, kipenzi changu, Media, bila kuwasahau nyinyi mashabiki wangu wapendwa kwani siku zote mmekuwa mkinisapoti bega kwa bega kwenye shida na raha…., Niwashukuru wasanii wenzangu toka ndani na nje kwani naamini changamoto tunazopeana ndio zimefanya hadi sasa muziki ufike hapa…hakika tuzo hizi si zangu bali ni za muziki wa Bongo fleva. Mwisho kabisa nimshukuru Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchango wake wa kila siku katika sanaa yetu!,,,Mr President your Son Did it !!!!!! Kwa upande wake Lady Jaydee aliandika: “Nashukuru wote mnaokubali kazi zangu, wote mnaosimama na kumtetea JayDee bila kusita, nashukuru kwa tuzo nyingine tena toka AFRIMMA. Wahenga walinena kuwa utavuna ulichopanda, mapenzi tele kwa kila mtu. Baaadhi ya wasanii walimpongeza Diamond kwa ushindi huo, akiwemo mpenzi wake, Wema Sepetu. Wengine waliompongeza Diamond kwa hatua hiyo ni msanii Linah Sanga, Aunt Ezekiel, Duly Sykes, Mwana FA, Linex na wengineo.
1
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Bashiru Ally amevitaka vyombo vya habari nchini kuandika, kuchambua, kutangaza kazi, fikra na maisha ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere miaka 20 baada ya kifo chake.Dk Bashiru alitoa mwito huo mjini Dodoma, alipokutana na wahariri na waandishi wa habari waliokuwa wanashiriki maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, yaliyofanyika kitaifa mjini hapa.‘’Vijana wengi wanamsikia Mwalimu Nyerere lakini hawamjui ni nani hasa na alifanya nini katika taifa letu na ukombozi wa nchi za Kusini mwa bara la Afrika,’’ alisema.Amesema wakati tasnia ya habari, itakuwa na jukumu la kuandika habari za uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu mwakani, sambamba na kazi hiyo pia waandike kazi za Mwalimu Nyerere, fikra zake na maisha yake ambayo yaligusa kila sekta ya maisha ikiwa ni pamoja na uchumi, siasa, elimu na ukombozi wa bara hili.Akijibu hoja na maswali ya waandishi katika kikao hicho, yakiwemo madai kwamba waandishi sasa hawana uhuru wa kufanyakazi kazi zao kama ilivyokuwa miaka ya nyuma na kwamba wanafanya kazi kwa hofu, Dk Bashiru amesema hatua zitachukuliwa kulikabili hilo ikiwemo kufanya majadiliano ya kero husika.Alipendekeza katika kukabiliana na hilo, apewe nafasi moja katika tume ya majadiliano kati ya serikali na vyombo vya habari, itakayoundwa kujadili viashiria vya kuminya uhuru wa vyombo habari ili ofisi yake iweze kushiriki katika majadiliano hayo.Aliwataka waandishi wa habari, kufanyakazi zao pasipo uoga, kwa kuzingatia weledi na maadili ya kazi zao na kwamba kazi ya habari si lelema.‘’Tuanze kujenga daraja kati ya waandishi wa habari, watumishi wa umma na vyama vya siasa. Niko tayari kukutana nanyi mara kwa mara. Mkipanga utaratibu mimi niko tayari kukutana nanyi,’’ aliwaambia wahariri hao waliokuwa wakiongozwa na Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Deogratias Balile.Balile kwa niaba ya wahariri, alimshukuru Dk Bashiru kukutana nao kwa mara ya kwanza na kuahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa lengo la kuwahabarisha Watanzania mambo yanayowagusa katika maisha yao.
3
MAKAMU wa Pili wa Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ramadhan Nassib, amefariki dunia jana na anatarajiwa kuzikwa leo kwenye makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.Taarifa kutoka familia ya Nassib inasema kiongozi huyo wa mpira alifikwa na umauti alfajiri ya kuamkia jana kwenye Hospital ya Taifa, Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.Taarifa ya familia kwa vyombo vya habari jana ilisema, msiba upo Manzese Tiptop na mwili utaswaliwa kwenye msikiti wa Mtoro kabla ya ku- pumzishwa makaburini Kisutu baada ya sala ya Ijumaa.Msiba huo umekuwa pigo kwa wadau mbalimbali wa soka, kila mmoja akimuelezea anavyomfahamu marehemu. Mara ya mwisho Nassib katika harakati za uongozi wa soka, aligombea nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2017 Dodoma, hata hivyo kura hazikutosha. Rais wa TFF, Wallace Karia amepokea kwa masikitiko taarifa za msiba na kutoa pole kwa wafiwa wote.“Nimepokea kwa masikitiko na mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Ramadhan Nassib hakika ni pigo kubwa kwa TFF kwa kuwa bado alikuwa na mchango mkubwa kwenye mpira wa miguu, kwa niaba ya TFF natoka pole kwa ndugu, jamaa na marafiki,” ilisema taarifa hiyo ya Karia kwa vyombo vya habari.
4
LYON, UFARANSA MSHAMBULIAJI wa timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo, amewataka mashabiki wa timu hiyo kujiandaa kushangilia ubingwa wa michuano ya Euro 2016 baada ya timu hiyo kuingia fainali ya michuano hiyo. Timu hiyo imeingia fainali baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Wales kwenye mchezo wa nusu fainali juzi, huku mchezaji huyo akifunga bao moja na kusababisha bao la pili. Staa huyo wa klabu ya Real Madrid, amedai kwamba Ureno ilianza katika mazingira magumu kwenye michuano hiyo tofauti na timu nyingine, lakini imefanikiwa kufika fainali na ina uwezo wa kutwaa taji hilo. Ronaldo amedai kwamba timu hiyo imefikia historia ya miaka 12 iliyopita ambapo iliingia fainali mwaka 2004 kwenye michuano hiyo lakini ilitolewa na Ugiriki. “Hii ni ndoto yetu ya kila mwaka kwa taifa letu, nadhani baada ya kumaliza fainali kila mmoja wetu atakuwa anacheka pamoja na machozi ya furaha kutokana na kile ambacho tutakifanya mbele ya mashabiki wetu. “Siku zote ndoto zangu zinasema kutwaa ubingwa nikiwa na taifa langu, naona ndoto hizo zinakaribia na ninaamini kila kitu kitakuwa sawa mwaka huu kwa kuwa uwezo wa kufanya hivyo tunao. “Siku zote ni vizuri timu ikaanza vibaya lakini ije kumaliza vizuri, ndivyo ilivyo na itavyokuwa kwenye mchezo wa fainali, kila mchezaji yupo kwa ajili ya kulitumikia taifa na ninaamini tupo tayari kufia uwanjani kwenye mchezo huo ujao. “Mashabiki wakae tayari kushangilia ubingwa msimu huu, hii ni nafasi ya pekee kutangaza ubingwa, hivyo mashabiki wakae tayari kwa hilo,” alisema Ronaldo. Hata hivyo, mchezaji huyo amedai kwamba Ureno si timu ya mtu mmoja kama watu wanavyodhani, ni timu ya wachezaji 11 hivyo kila mmoja anatakiwa kuonesha uwezo wake kwa ajili ya kupigania taifa lake. “Si lazima nifunge bao japokuwa kufunga ni jambo muhimu na zuri, ila kila mchezaji ana jukumu lake la kuhakikisha timu inafanya vizuri na inasonga mbele, si timu ya Ronaldo,” aliongeza. Bao la mchezaji huyo juzi lilimfanya aifikie rekodi ya mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa, Michel Platini, ambaye kwa sasa ni rais wa Uefa, nyota huyo alifunga mabao tisa hadi anamaliza soka lake mwaka 1984, wakati Ronaldo amefikisha idadi hiyo ya ufungaji bora wa miaka yote tangu pale alipoanza kucheza michuano hiyo mwaka 2004.
4
Twiga Stars ipo kambini Zanzibar kujiandaa na michezo ya Afrika (All African Games) inayotarajiwa kufanyika Congo Brazzaville mwezi ujao. Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Zanzibar jana, kocha Kaijage alisema timu yake inaendelea vema na maandalizi na anashukuru vijana wake wanashika anachowafundisha.“Nashukuru vijana wangu wananielewa vema, ninachosubiri kwa sasa ni mechi yetu ya kirafiki dhidi ya Kenya tu,” alisema. Ikiwa Zanzibar, Twiga inajifua kwenye viwanja viwili tofauti Amani na Fuoni. Mkuu wa msafara wa Twiga, Blassy Kiondo alisema timu ina morali hali inayowapa matumaini viongozi.Wakati huo huo, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Burundi (FBF), Reverien Ndikuriyo kwa kuchaguliwa kuwa spika wa Bunge la Seneti nchini humo.Katika salamu hizo za pongezi kwa Rais wa FBF na nakala zake kwenda CECAFA, CAF na FIFA, Malinzi ameelezea imani yake kwa Seneta Ndikuriyo na amemtakia kila la heri na mafanikio katika nafasi hiyo mpya aliyochaguliwa.
4
MKURUGENZI wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), Robert Kisena (46) na wenzake watatu, wamefi kishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka 19 likiwamo la kuisababishia mradi huo hasara ya Sh bilioni 2.4 na utakatishaji fedha.Mbali na Kisena, washitakiwa wengine ni Kulwa Kisena au Simon Kisena (33), mkazi wa Kibada wilayani Kigamboni na mfanyabiashara, Charles Newe (47), Mhasibu wa UDART na mkazi wa Mjimpya Kibamba na Chen Shi (32), mfanyabiashara na mkazi wa Masaki. Washitakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na kusomewa mashitaka na Mawakili wa Serikali, Ester Martin na George Barasa.Washitakiwa wote kwa pamoja, wanadaiwa Mei 25,2015 na Desemba 31, 2016 maeneo ya Dar es Salaam, kwa makosa yao waliisababishia UDART hasara ya Sh 2,414,326,260.70. Washitakiwa hao hawakuruhusiwa kujibu chochote, kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo. Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 25, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Washitakiwa walipelekwa rumande kwa sababu mashitaka yao hayana dhamana. Katika mashitaka ya kwanza inadaiwa kuwa kati ya Januari Mosi, 2011 na Mei 31, mwaka jana maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam kwa pamoja na wenzao, ambao hawako mahakamani waliongoza kundi la uhalifu.Inadaiwa Januari Mosi 2015 na Desemba 31, 2017, maeneo ya Jangwani wilayani Ilala, Kisena na Kulwa wakiwa wakurugenzi wa kampuni iliyojulikana kwa jina la Zenon Oil and Gas Limited, walitengeneza kituo cha mafuta bila ya kupata kibali kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA). Katika mashitaka ya tatu yanayowakabili Kisena na Kulwa, inadaiwa katika tarehe hizo maeneo ya Jangwani, walifanya biashara ya kuuza mafuta eneo lisiloruhusiwa, linalojulikana kama yadi ya mabasi yaendayo haraka ya Jangwani.Pia inadaiwa Kisena, Kulwa na Newe kati ya Mei 25,2015 na Desemba 31, 2016 wakati mshitakiwa wa kwanza na wa pili wakiwa wakurugenzi wa Kampuni ya Mabasi yaendayo Haraka (UDART PLC) na mshitakiwa wa tatu akiwa mhasibu, waliiba mafuta yenye thamani ya Sh 1,216,145,374.10 mali ya UDART. Katika mashitaka ya tano na sita, inadaiwa washitakiwa hao watatu kati ya Mei 25,2015 na Desemba 31, 2016, walitakatisha Sh 1,216,145,374.10 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu.Katika mashitaka ya kughushi, inadaiwa Kisena na Shi, Oktoba 20, 2012 katika maeneo yasiyojulikana jijini Dar es Salaam, walighushi nyaraka iliyojulikana kama Extract Board Resolution ya tarehe hiyo kwa lengo la kuonesha kuwa Kampuni ya Longway Engineering, imefungua akaunti ya benki ya KCB, kitu ambacho siyo kweli. Washitakiwa hao pia wanadaiwa tarehe hiyo hiyo, ya Oktoba 20,2012 maeneo ya Benki ya KCB tawi la Oysterbay wilayani Kinondoni, walitoa nyaraka za uongo ya Extract Board Resolution kwa benki hiyo kwa lengo la kuonesha kuwa wanachama wa Kampuni ya Longway Engineering, wameamua kufunguliwa kwa akaunti hiyo, kitu ambacho siyo kweli.Oktoba 20,2012 maeneo yasiyojulikana, Kisena na Shi walighushi nyaraka inayoonesha idadi ya wabia ya tarehe hiyo, lengo kuonesha kuwa watu walioorodheshwa ni wabia wa Kampuni ya Longway Engineering na kwamba wana mamlaka ya kufungua akaunti kwa benki hiyo. Kisena na Shi wanadaiwa Aprili 6,2016 maeneo ya Benki ya NMB, walighushi na kutoa nyaraka inayoonesha ya maombi ya kutuma fedha, lengo ni kuonesha kuwa Sh 549,925,000 yalikuwa malipo kwa Kampuni ya Longway Engineering ya kutengeneza vifaa vya umeme na usimikaji wake, kitu ambacho sio kweli.Pia inadaiwa washitakiwa hao Juni 8, 2016 maeneo ya Benki ya NMB, walijipatia kwa njia ya udanganyifu Sh 549,925,000 kutoka UDART kwa kudanganya kuwa fedha hizo zilikuwa malipo kwa Kampuni ya Longway Engineering. Wanadaiwa Aprili 8, 2016 maeneo ya Benki ya NMB, walitakatisha fedha Sh 549,925,000 kutoka kwenye akaunti ya NMB inayomilikiwa na Shirika la Usafiri Dar es Salaam-Mradi wa Dart kwenda akaunti ya KCB, wakati wakijua fedha hizo ni zao la kughushi.Kisena na Shi wanadaiwa Mei 26, 2016 maeneo ya Benki ya NMB, walighushi na kuitoa fomu kwa benki hiyo lengo la kuonyeha Sh 750,000,000 yalikuwa malipo kwa kampuni hiyo kwa ajili ya kutengeneza vituo vya mabasi hayo vya Kimara, Feri, Ubungo na Morocco, kitu ambacho sio kweli. Martin alidai kuwa washitakiwa hao pia Juni 9, 2016 katika benki ya NMB, walijipatia Sh 603,255,886.58 kutoka UDART kwa kudanganya kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo. Pia wanadaiwa walitakatisha fedha hizo, ambazo walizitoa katika akaunti ya UDART kwenda Benki ya KCB.
3
VIJANA zaidi ya 500 wameunganishwa na shirika linalojikita kupeleka misaada ya kifedha kwa wasomi, wabunifu na wafanyabiashara ndogo la World Business Angels Investment Forum (WBAF) ili kuwasaidia kifedha na kufi kia malengo yao ya kibiashara.Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Wawekezaji Malaika Tanzania, Sabetha Mwambenja alisema shirika hilo lisilo la kiserikali ndio jukwaa la kuwafikia Watanzania wabunifu, wavumbuzi na wanaoanza biashara kufuatia ubunifu wao na kuwasaidia wafanyabiashara wadogo. Mwambenja alisema lengo la kuwaunganisha vijana hao ni kuwawezesha kushiriki kinyang’anyiro cha kuwapatia mtaji watu 66 watakaofanya vizuri baada ya kuwasilisha mawazo yao ya biashara.Alieleza kuwa wajibu wa shirika hilo ni kutoa mitaji, kuwalea wahusika mpaka kufikia hatua ya kusimama kibiashara, kuwaunganisha na masoko ya huduma na bidhaa walizobuni na kuwapa taarifa zinazohusu bidhaa zao kidunia. “Tumeshafanya mazungumzo na sekta binafsi na za umma ikiwa ni pamoja na Tume ya Sayansi (Costech), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Mtakatifu Josefu, Chuo cha Tumaini Dar es Salaam (Tudarco) na Taasisi ya Teknolojia (DIT),” alisema Mwambenja.Alisisitiza kuwa WBAF imeshafungua milango kuwawezesha walengwa kutuma maombi kwa Shirika la Malaika ili waunganishwe kupitia kamati ya uwekezaji ambayo itapokea miradi na kuchuja. Alifafanua kuwa mkutano utakaotaja washindi utafanyika February 20, mwakani Istanbul nchini Uturuki.Alieleza kuwa WBAF imeamua kujikita kulisaidia kundi hilo kufuatia kilichobainika kuwa wametengwa na taasis za fedha huku wakishindwa kukopesheka kutokana na kushindwa vigezo vya riba na kukosa dhamana. Pia alisema WFBA inafanya kazi katika nchi 66 duniani katika mabara yote Afrika na Ulaya. “Shirika la wawekezaji malaika limechaguliwa na WBAF inayoshirikiana kufanya kazi kwa pamoja na idara mojawapo katika kundi la nchi zinazoendelea kiviwanda duniani maarufu kama G20,” alisisitiza Mwambenja.
3
Patricia Kimelemeta, Dar es Salaam Serikali imetoa maboksi 40 ya vifaa vya kujifungulia kwa wajawazito watakaojifungua katika kipindi cha Sikukuu ya Pasaka Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salam leo Alhamisi Machi 29, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk. Grace Maghembe amesema vifaa hivyo vitasambazwa kwenye baadhi ya vituo vya afya na zanahati zilizopo katika Halmashauri tano za mkoa huo ili waweze kupatiwa wajawazito watakaojifungua katika kipindi hicho. “Lengo la serikali ni kuboresha huduma za afya ikiwamo afya ya mama mjamzito na watoto wachanga wenye umri chini ya miaka mitano, ndiyo maana serikali imetoa vifaa hivi ili kuhakikisha wajawazito wanajifungua salama,” amesema Dk. Maghembe. Amesema vifaa hivyo vitasambazwa kwa waganga Wakuu wa halmashauri hizo ili waweze kuvipeleka kwenye vituo vilivyotagwa Kwa ajili ya kuvigawa Kwa wahusika. Alisema Kwa upande wa Kigamboni, vifaa hivyo vitapelekwa kwenye vituo vya Kigamboni, Vijibweni na Temeke vituo vya Temeke wakati Halmashauri ya Ilala watapewa vituo vya Kinyerezi, Kitunda, Pugu na Buguruni. Katika mgawo huo, amesema kila zahanati itapewa boksi nne ambazo ndani yake kuna vifaa 40 Vya kujifungulia. “Ukienda kununua kwenye maduka ya dawa, kifaa kimoja kinauzwa zaidi ya 150,000, lakini tumeamua kutoa zawadi Kwa kuwapa vifaa bure wanawake wote watakaaojifungua kipindi cha pasaka,” amesema.
3
Huduma hiyo ilizinduliwa Dar es Salaam mwanzoni mwa mwaka jana na baadaye ilisambazwa kwenye mikoa ya Arusha, Tanga, Dodoma na Morogoro na hivyo kuufanya mtandao wa 4G kuwa mpana na wa kasi nchini Teknolojia ya 4G LTE ina kasi ya nguvu takribani mara tano ikilinganishwa na teknolojia ya 3G inayotumiwa na watoaji wengine wa huduma hiyo kwenye soko la Tanzania.Mtandao wa 4GLTE una kasi kubwa kwenye kusambaza na kupakua vitu mbalimbali kutoka kwenye intaneti pamoja na kupiga miito ya simu ya skype.Hali kadhalika inawezesha wateja kwa kiwango kikubwa kuwa na uzoefu wa kutiririsha video au kufanya mikutano na inaweza kuhimili kutumika kwenye kupata video, mikutano, mwonekano wa hali ya juu, blogu za video, michezo mbalimbali na kupakua video kwenye mitandao ya kijamii.Ofisa Biashara Mkuu wa Tigo, Shavkat Berdiev alisema katika taarifa kwa vyombo vya habari kuwa mipango ya kupanua teknolojia ya 4G hadi kwenye maeneo yote nchini, inafanyika ikiwa ni mkakati wa kampuni hiyo wa kuwapatia wateja wake huduma ya hali ya juu duniani ili kuwawezesha kuendesha maisha ya kidigitali.Tangu mwaka jana, Tigo ilishawekeza Dola za Marekani milioni 120 kwa mwaka kwenye upanuzi wa mtandao wake pamoja na kuboresha maeneo ya mitandao ya 4G na 3G na Mkongo wa Mawasiliano.Hali kadhalika kuongeza idadi ya kufikiwa kwa huduma kwa wateja nchi nzima. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) takribani asilimia 67 ya idadi ya watu wazima wanamiliki simu za mkononi, huku idadi ya watumiaji wa intaneti hadi mwaka 2014 ilikuwa imeongezeka kufikia watu milioni 9.3.
5
Safina Sarwatt – Moshi HOSPITALI ya Rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC), imesema iko kwenye mchakato wa hatua za kuanzisha maabara ya virusi vya korona ili kukabiliana na vizusi hivyo endapo itabainika kuwepo kwa mgonjwa wa korona.  Mkurugenzi wa Mtendaji wa KCMC na Katibu Mkuu wa Shirika la Msamaria Mwema la Tanzania, Professa  Gilearrd Masenga aliyesema hayo jana, wakati wa ibada ya shukrani ya maadhimisho miaka 49 tangu kuanzishwa kwa hospitali hiyo kuelekea miaka 50 . Professa Masenga, alisema hospitali tayari imetenga eneo maalumu kwa ajili kujenga maabara ya virusi vya korona.  Alisema hospitali imejipanga kwa vifaa tiba pamoja na watalaamu kwa ajili ya dharura, endapo itatokea mgonjwa mwenye virusi vya korona kwa kushirikiana timu ya mkoa.  “Tumejipanga kwa vifaa na watalaamu wetu wako tayari muda wote,tunashirikiana na hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi  na timu iliyondwa na ofisi ya mkuu wa mkoa, nawaondoa hofu wananchi kwamba tupo vizuri, “alisema professa Masenga.  Alisemakutokana na mkoa huo kuwa miongoni mwa mikoa ambayo inapokea wageni wengi kutoka nje ya nchi kwa sababu za utalii wa hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, umeimarisha huduma muda wote. Alisema  hospitali hiyo, ina madaktari na wauguzi wa ngazi mbalimbali, madaktari bingwa 76 ,madaktari wa kawaida 74 na madaktari wasaidizi wanne  na (Clinical officers) 6. Alisema kwa miaka 49, sasa kuelekea jubilee ya miaka 50 ,hospitali   imefanikiwa kupiga hatua kubwa katika fani ya kitabibu kwa kanda nzima ya kaskazini pamoja na taifa.  “Mafanikio haya yanatokana na jitihada za uongozi na  watumishi vitengo mbalimbali ndani ya hospitali ambao wamekuwa uti wa mgongo katika hatua tunazopiga siku baada ya siku, “alisema.  Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Fredrick Shoo aliipongeza hospitali hiyo kwa hatua kubwa waliyopiga katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi, ambapo aliwataka kuongeza juhudi zaidi  ili kuhakikisha kwamba wanaondoa changamoto ndogo ndogo zinazojitokeza. 
0
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda amesema wizara yake inataka kumpa zawadi Rais John Magufuli, kwa kufufua viwanda vyote, vilivyoanzishwa nchini na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.Aidha, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko chini ya timu ya pamoja ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Kilimo, imekusanya tani 221,060 za korosho ghafi zenye thamani ya Sh bilioni 718. Kakunda alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana. Alisema kwa sasa wameanza na kiwanda cha General Tyre, ambapo wanafanya tathimini kukifufua kwa ajili ya kutengeneza matairi.Alisisitiza wanataka kumpa zawadi Rais Magufuli kwa kuhakikisha wanafufua viwanda vilivyoanzishwa na Mwalimu Nyerere, kikiwamo kiwanda cha General Tyre. Akizungumzia korosho na viwanda, alisema serikali imekusanya tani 221,060 za korosho kutoka kwa wakulima. Kwamba serikali inaweka kipaumbele cha kutosha kwa viwanda mbalimbali ili kuimarisha viwanda vya ndani.Aliwataka wamiliki wa kampuni na watu binafsi, wanaotaka kununua korosho, wawasilishe nia yao kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara ili waseme wanahitaji kununua korosho za kiasi gani kwa bei ya Sh 3,300. “Tukisema yeyote anaweza kununua korosho tunamaanisha wenye maduka makubwa au wafanyabiashara wowote wale, kwani tunauza korosho kwa kiasi cha tani anazohitaji mnunuzi, hata kama ni tani 10 ili mradi tuelewane bei,” alisema.Alisisitiza kuwa bei watakayoelewana ni lazima izingatie kuwa wamenunua korosho hiyo kwa Sh 3,300 kwa kilo, gharama za usafirishaji kutoka shambani hadi kwenye chama cha msingi na gharama za upakuaji na upakizi, sambamba na malipo ya tozo za kisheria za halmashauri na nyingine ikiwemo kuchangia elimu.Kuhusu kampuni iliyonunua koroshoAkizungumzia mnunuzi aliyenunua korosho kutoka nchini Kenya wa Kampuni ya Indo Power Solution, alisisitiza serikali haisikilizi maneno ya watu, bali inafanya biashara kulingana na mikataba waliyokubaliana. Alisema hivi sasa kampuni hiyo, inaendelea kukamilisha taratibu za kisheria na kibiashara na ikikamilisha taratibu hizo, atapewa shehena yake ya tani 100,000 yenye thamani ya Sh bilioni 418.Pia, alisema mnunuzi mwingine wa kampuni ya Bi-Southern ya nchini Tanzania, atasaini mkataba wa kununua tani 15,000 baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia mkataba na maelekezo ya kisheria yatakapokamilika. Wakati huohuo, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga amesema kwa mujibu wa sheria, wafanyabiashara wote wa korosho wanatakiwa wawe wamesajiliwa na kuwa na leseni ya biashara, hivyo wasiotekeleza sharti hilo, wanapaswa kuchukulia hatua kali za kisheria.Alisema hayo yamebainishwa katika Sheria ya Korosho Kifungu cha 12 ambacho hakimruhusu mtu yeyote kufanya kazi ya korosho bila kutambulika, ambapo pia Kifungu cha 15 cha sheria hiyo katika kifungu kidogo cha nne kinawataka wahusika wote wa korosho wawe wamesajiliwa na kuwa na leseni ya biashara hiyo. Kutokana na sheria hiyo, alisisitiza kuwa katika kulipa wakulima wa korosho, serikali haitamlipa mfanyabiashara asiyetambulika kisheria (Kangomba).Hasunga alisema hayo juzi wakati akizungumza na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Pwani. Alisema ni lazima sheria zifuatwe katika utekelezaji wa majukumu yote, ikiwemo biashara ya zao la korosho ili kuwanusuru wakulima wanaotumia nguvu nyingi katika kilimo hicho huku wakipata matokeo duni kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wanaowahujumu.
3
ADAM MKWEPU NA MITANDAO LIVERPOOL  haina jeuri tena ya kuweka rekodi ya kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu England  bila  kufungwa, badala yake imewapa nafasi Manchester City kuwa na matumaini ya kulitetea taji hilo hadi mwisho wa msimu. Katika mchezo wa 21 wa Ligi Kuu England, Liverpool imeruhusu kufungwa mabao 2-1 na Manchester City, hivyo haitaweza kufikia rekodi ya Arsenal ya msimu wa 2003/04 ambao walikuwa mabingwa bila kufungwa. Liverpool inaongoza ligi ikiwa na  pointi 54 wakati Manchester City ikipaa hadi nafasi ya pili na pointi 50, baada ya timu zote kucheza michezo 21 na kufanya  ubingwa wa ligi hiyo kuwa wazi kwa timu tatu za juu ikiwamo Tottenham yenye pointi 48 ikiwa na  idadi sawa ya michezo iliyochezwa na vinara hao. Historia imeweka wazi kuwa timu inayoweza kufikisha pointi 50 hatua kama hii inaweza kunyakua taji hilo. Kitendo hicho kilionekana kwa Chelsea ilivyonyakua taji hilo msimu wa 2005/06, Manchester United msimu wa 2006/07 na Manchester City 2017/18. Kama Liverpool  ingeshinda  dhidi ya Manchester City wiki iliyopita katika Uwanja wa Etihad,  kusingekuwa na nafasi  kwa  timu nyingine kuwaza ubingwa huo  msimu huu kwa kuwa ingekuwa na  tofauti ya pointi 10 dhidi ya miamba ya Manchester. Lakini kwa  sasa ubingwa wa ligi hiyo itategemea na matokeo ya  michezo 17 iliyobaki, ndivyo historia inavyoeleza namna gani itakavyokuwa ikiwa matokeo yatakwenda kama yalivyotokea wiki iliyopita. Ni miaka 28 tangu Liverpool itwae ubingwa wa ligi hiyo na wengi watakumbuka namna ilivyokosa kunyakua taji hilo  msimu wa 2013/14 wakati timu hiyo ikiwa chini ya kocha Brendan Rodegers. Baada ya kucharazwa na Chelsea taratibu iliondoka katika mbio za ubingwa na kuiachia Manchester City. Ni muhimu kukumbuka tukio hilo licha ya kwamba Liverpool kwa sasa ipo katika ubora wa hali ya juu. Tukio kama hilo lilitokea  msimu wa 1996/97 wakati Liverpool ikiwa chini ya Roy Evans na ikamaliza nafasi ya nne ikipitwa pointi saba na bingwa Manchester United iliyokuwa ikifundishwa na Sir Alex Ferguson. Wakati huo kama kikosi cha Evans kingepata pointi nne katika michezo miwili kingeongoza msimamo wa ligi hiyo. Kwa sasa Liverpool inatakiwa kuwajibika kuhakikisha pengo la idadi ya pointi iliyopo haipungui na kuwapa nafasi wapinzani wake. Timu hiyo kwa sasa ipo kwenye presha ya kuhakikisha inafanya vizuri katika kila mchezo na pengine jambo hilo linaweza kuwagharimu kutokana na upinzani uliopo kwenye ligi hiyo. Moja ya sababu ya Liverpool kucheza michezo 20 bila kufungwa ilitokana na ubora wao, hiyo inawafanya kuwa bora Ulaya na pengine duniani kwa sasa. Ili kufanikiwa ilichokifanya katika michezo 20 iliyopita, Liverpool inatakiwa kutokata tamaa kuamini kwamba waliteleza na wanatakiwa kuinuka tena katika ubora wao. Majogoo hao bado hatima ya ubingwa wa England upo kwenye  mikono yao, lakini wakiteleza tu itakuwa imekula kwao. Taji kubwa ambalo Liverpool imelinyakua kwa sasa ni Kombe la FA msimu wa 2005/06. Baada ya kumaliza msimu uliopita ikiwa nafasi ya nne ikitoka kupoteza mchezo wa fainali wa Ligi ya Mbaingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid, imejaribu kuongeza nguvu kikosi chao kwa kusajili wachezaji kadhaa lakini wengi wao wanahitaji uzoefu. Kikwazo kingine kinachonekana kwa Liverpool msimu huu ni wakati itakapokutana na Brighton, Crystal Palace , Leicester, West Ham, Bournemouth. Februari 24 mwaka huu timu hiyo itavaana na Manchester United, ikiwa ni siku chache baada ya kucheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya  Bayern Munich. Mzunguko wa pili Liverpool ilishinda dhidi ya Manchester United katika hali ya kutokuwa na presha lakini  kwa sasa mambo yamebadilika tangu  Jose Mourinho afukuzwe na nafasi yake kuchukuliwa na Ole Gunnar Solskjær. Lakini  zaidi ni kwamba Manchester United wanatakiwa kuwa katika kiwango cha juu wakati wakivaana na PSG wiki moja kabla ya kuvaana na Liverpool. Wakati huo Manchester City na Tottenham bado ratiba zao hazitakuwa na  presha, kwani vijana wa Pep Guardiola watakuwa wakivaana na Everton huku Tottnham ikivaana na  Burnley katika Uwanja wa Turf Moor. Wiki moja baada ya kucheza dhidi ya Manchester United na siku chache baada ya kucheza dhidi ya Watford, ikiwa katikati ya wiki Liverpool itavaana na Everton katika Uwanja wa Goodison Park. Liverpool inayo rekodi nzuri katika uwanja wa nyumbani uliopo mji mdogo wa  Merseyside wakati inapocheza dhidi ya wapinzani wake, lakini inapotokea  kucheza katika eneo tofauti matokeo yanakuwa tofauti pia. Kwa Manchester City na Tottenham, zitakuwa zikivinjari huku wakitaka Liverpool ipoteze mchezo huo. Lakini Manchester City italazimika kuifunga Bournemouth katika mchezo utakaochezwa Uwanja wa Vitality, wakati Tottenham ikiwa nyumbani ikitafuta pointi dhidi ya Arsenal. Liverpool itavaana na Tottenham katika Uwanja wa Anfield Machi 30 mwaka huu,  hii ikiwa nafasi kwa Manchester City kuongoza ligi kwa mara nyingine. Msimu uliopita vijana wa Klopp walifungana mabao 2-2 dhidi ya  Tottenham na hiyo inaonekana huenda ikatokea tena msimu huu katika hatua hii ya mzunguko wa pili.Wakati mchezo huo ukiendelea, Manchester City itakuwa ugenini ikicheza dhidi ya Fulham. Kwa sasa Fulham ipo chini ya kocha mpya, Claudio Ranieri, huenda akabadilisha matokeo ya awali ambapo timu hiyo ilifungwa mabao 3-0 katika Uwanja wa Etihad. Liverpool itamaliza presha ya michezo mikubwa wakati itakapovaana na Chelsea Aprili 13 mwaka huu. Miamba hiyo katika michezo yao iliyopita ilifungana bao 1-1 wakati zilipovaana Uwanja wa Stamford Bridge na matokeo hayo yanaweza kuzifurahisha tena klabu za Manchester City na Tottenham. Katika wiki hiyo hiyo, Manchester City itakuwa ugenini ikicheza dhidi ya Crystal Palace. Mchezo uliopita vijana wa Guardiola waliwafunga Palace mabao 3-2 katika Uwanja wa Etihad Desemba 22 mwaka huu huku Tottenham ikicheza dhidi ya Hudderfield.
4
WANAFUNZI 214 wa shule za msingi na sekondari mkoani Kilimanjaro, wamekatishwa masomo kutoka na kupewa ujauzito kwa kipindi cha Januari hadi Septemba, mwaka huu.Mkuu wa Mkoa, Anna Mghwira alisema hayo juzi wakati akizungumzia tatizo la mimba shuleni kwa mkoa huo na hatua zinazochukuliwa kudhibiti hali hiyo. “Mathalani mwezi Septemba mwaka huu watoto wapatao 60 wa Shule ya Sekondari ya kutwa ya Hai walibainika kujihusisha na masuala ya ngono jambo ambalo ni kichocheo kikubwa cha kuwapo kwa mimba mashuleni,” alisema.Alisema kutokana na hali hiyo, Bodi ya Shule ya Hai, ilifanya maamuzi ikiwemo kuwasimamisha masomo baadhi ya wanafunzi wakaidi zaidi na wengine wakihamishiwa shule nyingine.Mghwira alisema kwa mujibu wa uchunguzi wa wataalamu wa mkoa, moja ya sababu ya mimba mashuleni ni kukithiri kwa mmomonyoko wa maadili katika jamii. “Tatizo la mimba mashuleni linachangiwa zaidi na kuporomoka kwa maadili na baadhi ya wazazi/walezi kutotimiza wajibu ama majukumu yao katika malezi ya watoto wao wa kiume na wakike,” alisema.Mkuu wa Mkoa alisema miongoni mwa jitihada zilizofanyika katika kukabiliana na vitendo hivyo ni ushirikishwaji wa wadau wa elimu katika kupanga mikakati ya kudhibiti matukio ya mimba mashuleni.Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Moshi, Maulid Meshak na Mwanaima Msangi, walisema mimba mashuleni zinaweza kupungua iwapo wananchi watajenga mabweni katika shule ambazo wanafunzi hutembea umbali mrefu kwenda shule.“Uhamasishaji ufanyike ili yajengwe mabweni ya kutosha kwa wanafunzi wanaoishi mbali na zilipo shule, kinyume na hapo mimba zitaendelea kuwepo” alisema Msangi. Wananchi hao walitaka kuwapo kwa taarifa za mara kwa mara kuhusu hatua zinazochukuliwa kwa watu wanaopatikana na hatia ya kuwapa wanafunzi mimba ili iwe fundisho kwa wengine.
3
UJENZI wa Reli ya Kisasa (SGR) awamu ya kwanza Dar es Salaam hadi Mwanza kilometa 1,219, umetajwa kuwa licha ya kuzalisha ajira, pia utaongeza ufanisi wa usafiri na usafirishaji na kupunguza gharama za usafirishaji abiria na mizigo, utachochea uanzishwaji wa viwanda na ukuaji kwa kasi kwa miji midogo.Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge wakati akikagua ujenzi wa stesheni ya Gulwe wilayani Mpwapwa, Meneja Msaidizi wa Mradi wa SGR, Christopher Mangwella alisema, “SGR ikikamilika itachochea mipango ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kutekeleza sera ya viwanda na kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo 2025.”Mang’wella alisema reli itachochea mapinduzi ya uchumi kwa kanda nzima ya Afrika Mashariki na Kati hususani nchi zisizopakana na bahari. Alisema ujenzi wa njia hiyo umegawanyika katika vipande vitano, lakini vipande viwili vya Dar es Salaam hadi Morogoro (kilometa 300) na Morogoro hadi Makutupora, Singida (kilometa 422) utakamilika Februari, 2021. “Vipande vingine ni Makurupora-Tabora (kilometa 376.5), Tabora-Isaka (kilometa 162.5) na Isaka-Mwanza (kilometa 311.25) utaendelea kwa awamu hadi kukamilika,” alisema.Alisema kwa sasa kazi zinaendelea katika vipande viwili vya kwanza vyenye jumla ya kilometa 722 ambazo njia kuu ni kilometa 541 na njia za kupishana kilometa 181 zenye uwezo wa kubeba mizigo tani 35 kwa ekseli na mwendokasi wa kilometa 160 kwa saa. Alisema kipande cha Dar- Moro kinajengwa kwa ubia wa Kampuni ya Yapi Merkezi ya Uturuki na Mota-Engilya ya Ureno, lakini kipande cha Morogoro-Makutupora kinajengwa na Kampuni ya Yapi Merkezi peke yake.Wahandisi washauri wa mradi anayesimamia kwa niaba ya serikali ni Kampuni ya KORAIL JV ambayo ni ubia wa kampuni nane za KORAIL, CHEIL na DMEC kutoka Korea, MULTITECH kutoka Botswana, BARAJI kutoka India, SSF kutoka Ujerumani, RINA kutoka Italia na UNITEC ya Tanzania. “Mradi huo utakagharimu Sh trilioni 7.1 za walipa kodi nchini, zimegawanyika katika vipande viwili kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro ni Sh trilioni 2.7 na kipande cha Morogoro-Makutupora ni Sh trilioni 4.4,” alisema.
3
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewahukumu kulipa fidia ya Sh milioni 6.8 na kuwaachia huru kwa masharti washitakiwa watatu, kwa mashitaka ya kukutwa nyara za serikali wakiwemo tausi waliokuwa Ikulu.Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salumu Ally baada ya washitakiwa hao, David Graha, Mohamed Waziri na Mohamed Ally, kukiri kosa na kuingia makubaliano na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).Kabla ya hukumu hiyo kusomwa, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon aliwasilisha mbele ya hakimu huyo nyaraka za kibali cha DPP kuridhia mahakama hiyo kusikiliza na kutoa hukumu ya kesi hiyo kwa mujibu wa sheria.Simon pia aliwasilisha nyaraka za makubaliano ya DPP na washitakiwa hao yaliyofanyika Septemba 28, mwaka huu, huku akiomba mahakama iwafungulie mashtaka washtakiwa hao na kutoka hukumu kwa mujibu wa sheria.Alidai katika makubaliano hayo, washtakiwa waliondolewa mashtaka manne kati ya matano yaliyowakabili na kubaki na mashtaka ya kujihusisha na biashara ya nyara za serikali ambayo ndiyo waliyohukumiwa nayo.Katika mashitaka mapya ya kujihusisha na biashara ya nyara za serikali, ilidaiwa kuwa Juni 1, 2015 na Septemba 14, 2019 jijini Dar es Salaam washtakiwa hao walikutwa na ndege aina ya tausi watatu wenye thamani ya Sh milioni 3.4.
3
  Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA MGANGA wa Tiba asilia, Ashura Mkasanga (33), anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma akituhumiwa kumuua Mariamu Saidi (17), mkazi wa Mkoa wa Kigoma kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili kisha kukichoma moto. Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, alisema mwili wa marehemu ulikutwa kwa mganga huyo katika Kitongoji cha Chang’ombe, Kijiji cha Chamwino Ikulu wilayani Chamwino. Alisema mwili huo ulikutwa ukiwa umekatwa shingo kwa kutenganishwa na kiwiliwili na kichwa kikiwa kimechomwa moto na kubaki fuvu lisiloweza kutambulika sura yake. Kamanda huyo alisema baadhi ya sehemu za mwili wa marehemu ambazo ni mkono wa kushoto, shingo, kifua na sehemu za siri ziliunguzwa kwa moto. “Mnamo tarehe 8 mwezi huu majira ya saa nne usiku katika Kitongoji cha Chang’ombe, Kijiji cha Chamwino Ikulu, mtu mmoja mwanamke aliyefahamika kwa jina la Mariamu Saidi (17), mkazi wa Kigoma aliuawa kwa kukatwa shingo yake,” alisema. Kamanda Mambosasa alisema mazingira ya tukio hilo yanaonyesha kuwa mganga huyo asiye na kibali cha kuendesha shughuli za tiba asili, analaza wagonjwa nyumbani kwake, kufanya matambiko na kupiga ramli chonganishi. Alisema wamewakamata watu 11 wakiwamo wasaidizi wa mganga huyo ambao ni Victor Daniel (24) na mume wa mganga huyo, Noel Mazengo(30)
3
WABUNGE wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (AEAC) kutoka Tanzania, wameeleza njia muafaka ya kuondoa vikwazo visivyo vya ushuru katika jumuiya hiyo ni uanzishwaji wa kamati ya kusimamia biashara.Aidha, wabunge wamepongeza jitihada za serikali katika kuharakisha kupitisha makubaliano, yanayofanywa kwenye jumuiya hiyo, huku ikiwa makini katika kulinda maslahi ya nchi. Pia, wabunge hao wametaka Watanzania kujivunia nchi yao, kwa kuwa na amani, huku Rais John Magufuli akisifika kwa kuhakikisha rushwa inaondoka nchini. Wabunge hao wameitaka Tanzania kuenzi Kiswahili katika EAC na kuhakikisha wimbo wa jumuiya hiyo, unaimbwa katika shule za msingi.Walisema hayo walipozungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kabla ya kuanza ziara ya siku tano nchini Tanzania. Katika ziara hiyo, watakutana na wadau mbalimbali nchini ili kujua vikwazo, mafanikio na nini cha kufanya kwa watanzania katika kukamata fursa za kibiashara zilizopo katika mtangamano wa jumuiya hiyo.Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa waandishi wa habari, kabla ya kuanza ziara hiyo, walieleza bayana kuwa bado kuna changamoto kwa Watanzania kutambua na kukamata fursa zilizopo katika jumuiya hiyo. Mwenyekiti wa wabunge hao, Dk Abdullah Makame (pichani) alisema moja ya changamoto kubwa kwa watanzania na wananchi wengine ndani ya jumuiya hiyo ni kushindwa kuundwa kwa kamati ya kusimamia biashara EAC, ambayo ni utekelezaji wa Ibara ya 24 katika makubaliano ya Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja.“Kuundwa kwa kamati hii kutakuwa mwarobaini wa matatizo, kwani kutapunguza vikwazo visivyo vya kibiashara, kwani itifaki inazungumzia kuwa kila nchi inatakiwa kuwa na wajumbe watatu wenye utaalamu wa sheria na forodha, kwani kazi ya kamati hii kwa sasa inafanywa na mawaziri,“alisema. Alipongeza kazi za kukabili vikwazo zinavyofanywa na mawaziri, lakini kwamba ni vema kuwa na wataalamu.Alisema vikwazo hivyo siyo suala la kuvusha bidhaa pekee, bali pia binadamu kwenda katika nchi nyingine kupata ajira na kupata fursa mbalimbali. Makame alisema katika ziara yao iliyoanza jana, watakutana na wataalamu katika sekta binafsi na ile ya umma, kuona jinsi Tanzania inavyotekeleza makubaliano ya Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja pamoja na changamoto zake.Pia, watakutana na wanafunzi wa vyuo vikuu katika ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Aidha, watapata nafasi ya kukutana na asasi za kiraia, wananchi na wafanyabiashara katika Kituo Kikuu cha Mabasi ya kwenda mikoani na nchi jirani cha Ubungo, Dar es Salaam, ambapo watapata nafasi ya kutoa elimu kwa watanzania kuhusu mtangamano wa EAC.Wakizungumzia tuhuma zinazotolewa mara kwa mara na baadhi ya vyombo vya habari ndani ya EAC, kuwa Tanzania inakwamisha utekelezaji wa makubaliano kadhaa, Mbunge wa jumuiya hiyo, Adam Kimbisa alibainisha kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza, kwa kupitisha na kutekeleza mikataba mingi ya jumuiya hiyo. “Ni vema kueleza kuwa Tanzania ndiyo nchi kubwa katika EAC huku ikiwa ni mmoja wa waanzilishi, kuna baadhi ya maamuzi ni lazima kufanywa kwa umakini sana,” alibainisha Kimbisa.Mbunge mwingine wa jumuiya hiyo, Fancy Nkuhi alisema kuna baadhi ya masuala ya utekelezaji wa makubaliano, yanakuwa shida kutekelezwa kutokana na sheria kuwa tatizo, hivyo ni vema kufanyia kazi ili kurahisisha utekelezaji wake, kwani watendaji wanabanwa na sheria. Alitaka vijana kujitokeza katika mkutano, watakaofanya Jumatano jioni UDSM ili kufahamu namna ya kujiandaa kiutendaji na kutumia fursa zilizopo katika jumuiya.Mbunge Habib Mnyaa alisema Tanzania imejiweka mbali katika kuhakikisha umoja wa EAC unaimarika, kwa wimbo wake kuimbwa kwa ufasaha na watu wake, hivyo kutaka kuanza utaratibu wa kutumika katika shule za msingi. Alisema kwa sasa wimbo huo unaotumia lugha ya Kiswahili, hutumika katika nchi za Rwanda, Burundi na nyingine. Alisema pia bendera ya EAC ni vema ianze kupeperushwa katika wizara zote ili kujifahamisha na siyo kuwapa nguvu wengine.Alisema Tanzania ni mmoja wa waanzilishi wa EAC lakini nadra kuona bendera hiyo. Mbunge Ngwaru Maghembe alitaka watanzania kujivunia kuwa na amani katika ukanda huo. Alisema hivi karibuni walifanya ziara katika kambi za wakimbizi kwenye Jumuiya hiyo na ni Tanzania pekee ambayo haina wakimbizi kwenye makambi.Pia alieleza kuwa Tanzania inajivunia Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli ambaye anasifika katika ukanda huu katika kupambana na rushwa na amedhamiria kuiondoa nchini. Mbunge Pamela Maasay alitaka watendaji kuhakikisha kunakuwa na viwango sawa vya bidhaa katika EAC, ili kuwezesha wananchi kutoka pande zote kuvifuata na kunufaika. Kuhusu uanzishwaji wa Baraza la Vijana EAC, alisema muswada umepitishwa tayari na lengo ni kuwezesha vijana kukamata fursa mbalimbali.
3
Na Mwandishi Wetu, UNAPOKUTANA ana kwa ana na kijana Yuda Thadey, lazima nafsi yako itaurejea utukufu wa Mungu. Hakika hutoamini kwamba kijana huyo mlemavu aliyepooza kuanzia kiunoni hadi miguuni anafanya kazi nzito za ufundi ambazo si rahisi kufanywa na mtu wa kawaida tena mwenye elimu ya kawaida kama yeye. Kijana huyo anapatikana katika Wilaya ya Mwanga, Ugweno mkoani Kilimanjaro. Jina lake ni maarufu wilayani humo kutokana na kipaji alicho nacho. Akizungumza na gazeti hili, Thadey anasema kuna wakati anafanya kazi bila kulala. Wakati mwingine hutumia zaidi ya saa 20 kufanya kazi. Anasema anapoanza jambo lake hataki liishie njiani hivyo uhakikisha anamaliza ndipo huendelea na kitu kingine. Kijana huyo ni mahiri katika kutengeneza vifaa vyote vya umeme ikiwamo simu, kompyuta, redio na runinga. Pia anao uwezo wa kuhariri video na kurekodi, mtayarishaji wa muziki wa aina yoyote licha ya kwamba amebobea katika muziki wa Injili ambao anaupenda kwa sababu ameokoka. Anasema aligundua kipaji chake baada ya kuanza kutengeneza saa na baadae redio, ambapo kila siku alikuwa akichukua betri za redio na kugombezwa na mama yake. Anasema aliongezewa ujuzi wa vitu mbalimbali kutoka kwa jirani yao aliyejulikana kwa jina la Mzee Juma. “Nikiwa na Mzee Juma nilikuwa nikijifunza jinsi ya kutengeneza redio, lakini yeye alikuwa akitumia vifaa ambavyo si halisi hivyo, kwa sababu napenda kusoma nilisoma na kuvijua vile vya kitaalamu,” anasema. Anasema sasa hivi anajifunza masuala ya mtandao, hivyo huamka saa 12 asubuhi na kuamsha watoto kwa ajili ya kwenda shule baada ya hapo anaanza kutengeneza runinga au redio hadi saa 12 jioni, kisha anawasha kompyuta na kuanza kujifunza mambo mbalimbali ya intaneti. Akizungumzia fani anayoipenda anasema utangazaji ndio ilikuwa ndoto yake kuu na kwamba huenda ndiyo chanzo cha yeye kupenda ufundi wa redio na TV. Licha ya kutengeneza vifaa vya umeme, Thadey pia ni mwalimu wa muziki wa aina zote ambapo anatunga na kuimba, anapiga kinanda, gitaa na kurekodi japo kwa sasa anashindwa kwa sababu ana maumivu ya kifua. Anasema maumivu hayo yanatokana na kazi ya kufungua redio na televisheni. Hata hivyo, Thadey anasema anapotengeneza kompyuta, saa na vitu vingine huwa havimdhulu. Hivi majuzi alifanya kazi ya kuwarekodi wanakwaya wa kwaya ya Mtakatifu Theresia Kikweni Ugweno, ambao aliwatengenezea kuanzia ala na video huku akirekodi video hiyo kwa kutumia simu yake ndogo ya mkononi jambo lililowashangaza wengi. Kazi hiyo aliifanya katika mazingira magumu kwani walikosa hata chumba maalumu cha kuchukulia sauti pia hawakuwa na vipaza sauti hivyo alitumia akili ya ziada kwa kutengeneza mfumo ambao aliweza kuchukua sauti za wanakwaya wote kwa pamoja. Thadey anasema kurekodi bongo fleva ni rahisi zaidi kuliko kwaya. Thadey amekuwa ni mtu muhimu kwa wakazi wa Wilaya ya Mwanga kwani amekuwa akitoa elimu na ujuzi walionao kuwafunza vijana ili nao waweze kujiari kwa kutumia vipaji vyao. Thadey anasema alishawahi kutengeneza masafa ya Fm bila kujua na kuanza kupiga miziki yake. Anasema kuwa suala hilo lilitaka kumletea matatizo baada ya kuingiliana na masafa ya redio mojawapo nchini ambayo ilianza kukoroma na kutosikika vizuri. “Wahusika walinifuata kutaka kunikamata lakini walipoiona hali yangu wakanihurumia na kunielimisha kwamba kufanya hivyo ni kosa kisheria,” anasema. Anasema pia aliwahi kutengeneza simu ya mkononi kwa kutumia vifaa vyake na ikawa inafanya kazi vizuri. Anasema baada ya kuitengeneza aliijaribu kwa kuwapa vijana na kwenda umbali tofauti kasha kuwapigia simu ikawa inafanya kazi vizuri. Akatisha masomo Alizaliwa Novemba 9, 1973 akiwa mzima hana tatizo lolote. Alipokuwa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Kisanjuni, alianguka kutoka juu ya mti wa mzambarau, wakati akijaribu kuchuma zambarau. Hii ilikuwa mwaka 1985, baada ya kuanguka alipelekwa katika Hospitali ya Kifura mkoani Kilimanjaro. Kutokana na hali yake kuwa mbaya alikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa Kilimanjaro ya Mawenzi na kulazwa kwa muda wa miezi mitano, baada ya madaktari kubaini kuwa amevunjika uti wa mgongo. Baadaye alihamishiwa katika Hospitali ya KCMC, lakini kutokana uhaba wa fedha alirudishwa Mawenzi. Aliporudi nyumbani kwao Ugweno, madaktari walimshauri awe anahudhuria mazoezi katika Hospitali ya Mawenzi lakini alishindwa kutokana na kuvunjika mguu akiwa mazoezini. Thadey anasema; “nilishindwa kwenda hospitali baada ya kuvunjika mguu nikiwa nyumbani nafanya mazoezi kitandani,” anasema. Anasema baada ya hapo akapelekwa katika Hospitali ya Kifura na kulazwa kwa miezi minne. “Niliporuhusiwa kurudi nyumbani, baada ya mwaka mmoja nilivunjika tena mguu wa pili wakati naamka kitandani,” anasema. Thadey anasema kuwa huo ndio ulikuwa mwisho wa yeye kuendelea na shule licha ya kwamba alikuwa akiongoza darasani kwa kuwa mwanafunzi wa kwanza kuanzia darasa la kwanza hadi la tatu. Akiwa nyumbani baba yake aliamua kuendelea kumfundisha kusoma vitabu na magazeti jambo ambalo lilimsaidia kuwa mjuzi wa mambo mbalimbali.  Matatizo yamuandama Historia ya Thadey imejaa mikasa kwani hadi kufikia kuwa fundi anayetegemewa na wilaya nzima, aliwahi kumsababishia baba yake kufungwa mwaka mmoja katika gereza la Kilulu kwa kosa la kukutwa na nyaya za simu lakini mwenyewe anasema zilitegeshwa. Akizungumzia mkasa huo, baba mzazi wa Thadey, George Kajiru anasema kuna kijana ambaye aliiba redio kwa dada mmoja ambaye ni mwalimu aliyejulikana kwa jina moja la Rose na kumuuzia mwanawe kama spea na kwamba hakukuwa na kitu kingine zaidi ya hiyo. Baadaye Rose alibaini kuwa redio yake ipo kwa Thadey hivyo alitaka suala hilo liende polisi, ambao walipofika kumkagua wakaziona nyaya za simu, ikabidi waondoke na Kajiru. Anasema alipofika polisi alifunguliwa jarada na kesi ikapelekwa mahakamani ambako alikutwa na hatia akahukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela katika gereza la Kilulu. “Nilipomaliza kifungo baadaye ikabainika kuwa zile nyaya zilikuwa zimefichwa na mtu mwingine lakini kwa sababu tayari nilishatoka jela haikuwa na maana tena.  Afya mgogoro Thadey anasema kuwa licha ya kufanya kazi hizo, afya yake ni mgogoro kutokana na mazingira anayofanyia kazi, pia kazi anayoifanya ya kutengeneza vifaa vya umeme. Anasema kazi hiyo imemfanya aumwe kifua mara kwa mara kutokana na kuifanya huku akiwa amelala. Pia anasema kuwa huwa anasumbuliwa na ugonjwa wa UTI. “Hali hii inasababishwa na mpira ambao nimefungwa kwa ajili ya kujisaidia, hivyo dumu linalopokea haja ndogo likijaa na kukosekana mtu wa kuumwaga huwa unarudi katika mpira na hivyo kuniletea madhara,” anasema.  Changamoto za kikazi Thadey anasema kuwa kumekuwapo watu ambao huwakusanya walemavu na kuwaambia kuwa wanataka kuwapatia mikopo lakini haiwasaidii kutokana kwamba wanapewa kwenye makundi na hivyo inapotokea mmoja wao ameshindwa kulipa hujikuta wakiingia gharama zaidi. Anashauri taasisi za mikopo kuwafikia na kuzungumza nao kila mmoja kwa wakati wake na si kwa vikundi ili kujua hitaji la mtu na kuwakopesha mmoja mmoja ili kila mhusika abebe msalaba wake. Anataja changamoto nyingine kuwa ni kukatika kwa umeme na ulipaji wa bili kubwa huwa unamuumiza. Anasema ameshaomba mara kadhaa abadilishiwe mita na kupewa ya Luku bila mafanikio. Anasema anachokiwaza sasa ni kununua umeme wa jua kuwa kuwa utamrahisishia kufanya kazi bila kulipa gharama kubwa za umeme.  Ushauri Anawashauri mafunzi wenzie wapende kusoma ili kujua mambo mengi zaidi.  Ombi kwa Rais “Naomba Rais Dk. John Magufuli anisaidie nipate umeme wa jua hapa studio ili nifanye kazi zangu kwa ufasaha bila kuogopa gharama za umeme,” anasema na kuongeza: “Rais anataka Tanzania ya viwanda, ili atomize adhma yake  aanze na sisi vijana wenye ujuzi lakini hatuwezi kuuendeleza kwa kukosa fedha.”
0
Na Mwandishi Wetu KWAYA ya Wakorintho Wapili ya Wilayani Mafinga, mkoani Iringa, inatarajia kuzindua albamu yake ya Mchepuko sio dili kwenye tamasha la Krismasi linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama, amesema albamu hiyo ya Mchepuko sio dili ina nyimbo nane ambazo zinafikisha ujumbe  wa neno la Mungu kwa jamii. Msama alizitaja nyimbo hizo ni pamoja na Tanzania, Mchepuko sio dili, Watenda mabaya, Ee bwana, Yahwe tunakuinua, Tuokoe baba, Dunia hii na Hana. Aidha Msama alisema maandalizi ya kuelekea katika tamasha hilo yanaendelea vizuri, hivyo Watanzania wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kuelekea tamasha hilo. Aliongeza kuwa watanzania walichukilie tamasha hilo kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa Mungu baada ya kutupitisha katika kipindi kigumu cha uchaguzi Mkuu ambao ulifanyika kwa amani na utulivu ingawa kulikuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani. Msama alisema waimbaji wa Tanzania watakaosindikiza tamasha hilo ni pamoja na Rose Muhando, Upendo Nkobe, Joshua Mlelwa, Martha Mwaipaja, Jesca BM,  na Christopher Mwahangila, Sifael Mwabuka sambamba na Kwaya ya Yombo KKKT.  
1
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
NA TIGANYA VINCENT HALMASHAURI ya Wilaya ya Kaliua kuanzia Januari hadi Machi, mwaka huu, imenunua bandali 300 kwa gharama ya Sh milioni 80 kutokana na mapato ya ndani. Kauli hiyo, ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Haruna Kasele wakati wa kikao cha baraza la madiwani. Alisema bati hizo zitagawanywa kata zote ambazo zimekamilisha mabona, ununuzi wa mbao na vifaa kwa ajili ya upauaji. Alisema wanaendelea na ujenzi wa vyumba 6 vya maabara katika shule za sekondari za Kanoge, Kamsekwa, Zugimulole, Silambo, Seleli na Ilege. Katika hatua nyingine, Kasele alisema Kaliua imepokea Sh bilioni 1 kwa ajili ya mpango  wa elimu bila malipo kutoka Serikali kuu. Alisema kwa upande wa shule za msingi, wamepokea Sh milioni 683.9 na shule ya sekondari wamepokea Sh milioni 399.8. Aliishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo ambazo zimewawezesha wanafunzi kujiunga na shule za msingi na sekondari. Wakati huo huo,halmashauri hiyo imetoa mikopo ya Sh milioni 345 kwa vikundi mbalimbali. Alisema Sh milioni 133.5, zimetolewa kwa vijana, Sh milioni 184 zimetolewa kwa wanawake na milioni 27.5 zimetolewa kwa walemavu. Alivitaka vikundi ambavyo vimekopeshwa kuhakikisha wanarejesha fedha hizo ili ziweze kukopeshwa kwa vikundi vingine.
3
Na JANETH MUSHI-ARUSHA MWANAFUNZI Anna Zambi (16), aliyepoteza wazazi wake na wadogo zake watatu siku chache kabla ya kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, amesema anatamani kuwa mwanasheria ili aweze kusaidia watu wa makundi mbalimbali ikiwemo wanaofungwa kwa kuonewa. Anna aliyekuwa akisoma Shule ya Sekondari ya Wasichana yaMother Teresa of Calcuta ya mkoani Kilimanjaro, amefaulu kwa kupata daraja la pili na pointi 20. Akizungumza jana jijini Arusha na waandishi wa habari nyumbani kwa mama yake mdogo, Isabella Lyimo,  alisema anamshukuru Mungu kwa matokeo aliyoyapata japo ndoto yake ilikuwa kupata daraja la kwanza. “Nilikuwa na ndoto ya kufaulu vizuri zaidi na kupata daraja la kwanza ila nimepata la pili, namshukuru Mungu kwa matokeo haya. Wapo waliokuwa na matarajio ya kupata ufaulu mzuri ila wamekosa. “Tulikuwa jikoni tunasaidiana na dada kupika chakula cha mchana, mama mdogo akanipigia simu akaniambia matokeo yametoka, akaniuliza namba ya mtihani akaniambia nimefaulu kwa kupata daraja la pili, nilifurahi sana,” alisema.  MWANASHERIA Akizungumzia ndoto zake za baadaye, alisema anatamani kuwa mwanasheria ili kusaidia watu ikiwamo wanaobambikiwa kesi. Alisema anakumbuka enzi za uhai wa baba yake, aliwahi kuwa na kesi, hivyo na kuanzia hapo alitamani kuwa mwanasheria ili aweze kumtetea baba yake. “Nilitamani kuwa mwanasheria, awali baba alikuwa ofisa rasilimali watu katika moja ya taasisi Chalinze, alipata kesi ikafunguliwa mahakamani na alivyokuwa akirudi nyumbani alikuwa akilalamika kuwa kosa analokabiliwa nalo si la kweli, kuna hela zilihamishwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine.  “Baba alikuwa akisema angekuwa anajua sheria yasingempata yanayompata wakati huo. Na alituambia tuwe wanasheria ili ikitokea amerudishwa mahakamani tumsaidie. “Nakumbuka alipata kesi nikiwa darasa la saba, hukumu ilikuja kutoka kabla sijamaliza kidato cha nne na ndipo umauti ulipomkuta. Natamani kusaidia na wengine, kuna wanaofungwa kwa kuonewa,” alisema. SHULE ANAYOTAMANI KUSOMA Anna alisema anatamani kuendelea kidato cha tano na sita katika Shule ya Canossa iliyopo Dar ss Salaam. “Natamani kuendelea kidato cha tano Shule ya Canossa kwani naamini ni shule nzuri kitaaluma, hivyo mwanafunzi anavyosoma pale anakuwa na uhakika wa kufaulu,” alisema. Mwanafunzi huyo aliwaliza Watanzania baada ya vifo vya wazazi wake Lingston Zambi, Winifrida Lymo na ndugu zake Lulu, Grace na Andrew, Novemba 16, gari waliyokuwa wakisafiria kwenda kwenye mahafali yake ya kuhitimu kidato cha nne kutumbukia kwenye daraja lililokuwa limevunjika kutokana na mvua Handeni mkoani Tanga. Anna hakutaarifiwa msiba huo hadi alipomaliza mitihani na kurudi nyumbani kwao Dar es Salaam. Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa juma lililopita na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), katika Shule ya Mother Teresa Of Calcuta aliyosoma Anna, wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 121.  Kati ya wanafunzi hao, waliopata daraja la kwanza ni 12, daraja la pili 44, daraja la tatu 41 na daraja la nne 24.
3
Na YOHANA PAUL -MWANZA KAMISHINA wa Tume ya Uchaguzi Nchini (NEC), Jaji mstaafu Thomas Mihayo, amewataka watumishi wote waliopewa dhamana ya kusimamia uandikishaji na uboreshaji wa taarifa za wapiga kura kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga kura, kutekeleza jambo hilo kwa umakini na kwa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona. Jaji Mihayo aliyasema hayo jana jijini Mwanza wakati akifungua semina kwa mawakala waliopewa dhamana ya kusimamaia zoezi hilo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana mkoani hapa ambapo alisema kuanza kwa mchakato huo ni hatua za awali za kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba. Alisema uboreshaji wa taarifa za wapiga kura, utahusisha pia wasimamizi wa ndani na nje ya nchi hivyo dosari za aina yeyote zinaweza kulichafua taifa kuelekea uchaguzi mkuu na kuleta taswira ya tofauti.  “Tunapoenda kutekeleza jukumu hili tutambue kuwa suala la uboreshaji wa taarifa za wapiga kura ni la kikatiba na kidemokrasia na kwa kuwa nchi yetu inaongozwa kwa misingi hiyo, iwapo tutakamilisha mchakato huu kwa ufasaha itatupatia muongozo mzuri kuelekea uchaguzi mwaka huu. “Aidha nitumie nafasi hii kuwakumbusha wasimamizi wote mlioteuliwa kukamilisha zoezi hili, kuchukua tahadhari dhidi ya virusi vya corona kama inavyoelekezwa na Wizara ya Afya nasi kama NEC tumejipanga kutoa vifaa vyote vya kujikinga na tutatoa maelekezo kwa Watanzania jinsi gani wataweza kukamilisha zoezi hili kwa njia ya simu ili kuepusha misongamano,” alisema Jaji Mihayo. Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Thomas Rutachunzibwa, alisema wakati wa uboreshaji wa taarifa za wapiga kura kila mmoja achukue tahadhari dhidi ya corona pasipo kujali nafasi yake kwani ugonjwa huo hadi sasa hauna tiba. Pia aliwasisitiza wateule wa kusimamia zoezi la uboreshaji taarifa za wapiga kura wasitumie vibaya tahadhari ya corona kwani wapo wananchi watajihisi kama wananyanyapaliwa badala yake watoe maelekezo ya njia sahihi zitakazosaidia kujikinga kueneza virusi hivyo wakati wa utekelezaji zoezi hilo. Mkurugenzi Mkuu wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba aliwataka wasimamizi wa uboreshaji wa taarifa za wapiga kura kuvitunza vifaa watakavyotumia kwani vifaa hivyo vimenunuliwa na serikali kwa gharama kubwa sana.
3
Waamuzi hao watakaochezesha mchezo huo utakaoanza saa 10.00 jioni na kurushwa moja kwa moja na Kituo cha Televisheni cha Azam Tv kwa kushirikiana na Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC) ni Brian Nsubuga atakayepuliza kipenga na wasaidizi wake ni Bugembe Hussein na Katenya Ronald.Kamishna wa mchezo atakuwa Amir Hassan kutoka Somalia. Kocha Mkuu Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa atawakosa washambuliaji wake watatu katika kikosi ambacho kitaivaa Harambee Stars.Washambuliaji hao ni Mbwana Samatta kutoka KRC Genk ya Ubelgiji, Thomas Ulimwengu anayechezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na John Bocco ambaye ni majeruhi wa mguu aliumia wakati wa fainali ya Kombe la FA kati ya Yanga na Azam Jumatano wiki hii, Dar es Salaam.“Madaktari wamempa Bocco saa 72 za mapumziko. Bila shaka kabla ya kucheza na Misri atakuwa amepona,” alisema Mkwasa jana asubuhi na kuongeza kuwa Samatta ametuma taarifa kukosa mchezo dhidi ya Kenya kwa kuwa ana ratiba ya kucheza mchezo muhimu Mei 30, mwaka huu, lakini atajiunga na wenzake Jumatano kwa ajili ya mchezo na Misri Jumamosi.Kwa upande wa Ulimwengu, uongozi wa TP Mazembe nao waliomba kumtumia katika mchezo wa ushindani na mpinzani wake AS Vita. Pia kocha huyo anaangalia namna ya kuipanga vyema safu yake ya ulinzi baada ya kumkosa Kelvin Yondani anayetumikia adhabu ya kadi mbili za njano.Mabeki anaotarajia leo ni wale wa pembeni Juma Abdul na Mohammed Hussein, wakati katikati atawategemea Erasto Nyoni, Aggrey Morris na David Mwantika. Viungo waliopo na timu ni Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude, Farid Mussa na Shiza Kichuya.Washambuliaji ni Elias Maguli na Ibrahim Ajib, ambapo makipa ni Deogratius Munishi au Aishi Manula. “Nimeiandaa timu kucheza mifumo miwili ambayo ni 4-3-3 ambao ni mfumo wa ushambuliaji na pale tutakapokuwa tunazuia basi mfumo utakuwa ni 4-5-1,” alisema Mkwasa.Katika mchezo wa leo Mkwasa anayesaidiana na Hemed Morocco na Manyika Peter anayewanoa makipa atapata nafasi ya kubadili wachezaji hadi sita ambao ni utaratibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa mechi za kirafiki za kimataifa, pia makubaliano katika mkutano wa kabla ya mchezo.Stars iliwasili Nairobi, Kenya juzi asubuhi na kupokewa na wenyeji Shirikisho la Soka Kenya, ambako mchana kabla ya kwenda mazoezi ilitembelewa na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk John Haule. “Msaada wowote mnaotaka na chochote mnachohitaji tunaomba mtutaarifu tujue namna ya kuwasaidia. Msiwe na wasiwasi kabisa,” alisema Dk Haule.
4
BAADA ya kutolewa mapema katika michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita, Yanga inahamishia hasira zote kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mwadui ya Shinyanga utakaochezwa leo.Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kuanzia saa 1:00 usiku kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Katika michuano ya Mapinduzi iliyomalizika Zanzibar mwishoni mwa wiki iliyopita, Yanga ilitolewa hatua ya makundi baada ya kupoteza michezo miwili dhidi ya Azam (3-0) na Malindi (2-1) na kushinda miwili dhidi ya KVZ FC (1-0) na Jamhuri (3-1).Awali, Kocha Mkuu Mwinyi Zahera hakuipa kipaumbele michuano hiyo kwa kupelekea kikosi cha vijana, akisema nguvu kubwa wanawekeza katika michuano ya ligi na kuwapumzisha wachezaji tegemeo.Lakini kupoteza michuano ya Mapinduzi kulipokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki wa klabu hiyo, baadhi walifurahi na wengine kuchukizwa hivyo, huenda sasa baada ya kurejea kwenye ligi wakatumia nguvu ya kupambana kupata ushindi ili kufuta huzuni yao.Yanga inaingia kucheza dhidi ya Mwadui ikiwa inaongoza kwa pointi 50 baada ya kucheza michezo 18, kushinda 16 na kupata sare mbili.Ndio timu pekee, ambayo haijapoteza mchezo wowote mpaka sasa.Mwadui FC imeshacheza michezo 21, imeshinda sita, imepata sare sita na kupoteza tisa, ikiwa na pointi 24 katika nafasi 10. Timu hiyo ya Jangwani inapokuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani hujitahidi kufanya vizuri.Ubora wa wachezaji wake upo kila idara na yeyote ana nafasi ya kufunga akiwa katika nafasi nzuri.Mchezo huo utamkosa mshambuliaji hatari wa Yanga, Haritier Makambo anayeongoza kwa kufunga jumla ya mabao 11 akitumikia kadi tatu za njano.Makambo alikwenda kwao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa ajili ya matatizo ya kifamilia na alitarajiwa kuwasili jana, kwa mujibu wa mmoja wa wasemaji wa klabu hiyo Chicharito Anderson.Pia, itamkosa kipa wao Ramadhan Kabwili anayeuguza majeraha ya goti. Mwadui pia, sio timu ya kubeza na mara nyingi inapokutana na Yanga mchezo unakuwa wenye ushindani.Takwimu zinaonyesha katika michezo mitatu iliyopita Yanga imeshinda mmoja, Mwadui mmoja, na mchezo mmoja wamepata sare ya kutokufungana.Licha ya kutofautina pointi 26 bado haiwezi kuwa sababu ya kubezwa, matokeo yanaweza kupatikana kwa yeyote aliyejiandaa vizuri.Huenda Yanga ikapewa nafasi kubwa ya kushindana kutokana na ubora walionao mpaka sasa. Ila matokeo yoyote yanawezekana inategemea na mbinu za makocha wa timu zote mbili, ni nani atakayemuangusha mwenzake.
4
MKUU wa Mkoa wa Morogoro Dk Kebwe Stephen Kebwe amewatahadharisha Wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo vilivyotolewa na Rais John Magufuli vinawafi kia walengwa na si vinginevyo.Dk. Kebwe alitoa maagizo hayo wakati wa uzinduzi wa ugawaji wa vitambulisho 25,000 vya wafanya biashara wadogo uliofanyika juzi mjini Morogoro. “ Vitambulisho hivi viwafikie walengwa kama serikali ilivyokusudia kazi ya kuwagawia hao wahusika mione kama kaa la moto kwani nyie ndio wasimamizi wakuu kwenye maeneo yenu, sitarajii liende kinyume na maagizo,alisema Dk Kebwe.Mkoa wa Morogoro una wilaya saba ambazo ni, Morogoro, Kilosa, Kilombero, Mvomero, Gairo, Ulanga na Malinyi. Hivyo aliwataka kugawa vitambulisho hivyo bila upendeleo na vitolewe kwa kufuata maelekezo yaliyobainishwa.Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara wadogo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Faustini Francis alisema, jambo hilo ni jema alilofanya Rais na wako tayari kuchangia pato la serikali kwa kutoa ushuru kulingana na maelekezo yaliyowekwa
3
Akizungumza katika hafla ya utiaji huo wa saini iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Kamugisha Kazaura, alisema Mkataba huo una miradi itakayohusisha ujenzi wa mtandao wa teknolojia ya kisasa ya 4G, 3G na 2G.“Teknolojia hizi zitasaidia kampuni kupanua na kuboresha huduma zake nchi nzima na katika ubora wa hali ya juu, pia zitatoa huduma bora ya sauti na intaneti yenye kasi zaidi,” alisisitiza Kazaura.Alisema pia Mkataba huo utahusisha ununuzi wa mitambo kwa ajili ya kupeleka mawasiliano vijijini chini ya mpango wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF).Alisema kampuni hiyo kwa sasa imeshinda zabuni ya kupeleka mawasiliano katika kata 69 zinazojumuisha vijiji zaidi ya 400 vyenye wakaazi zaidi ya 500,000.“Chini ya mradi huo Mfuko wa UCSAF utaipatia TTCL dola za Marekani milioni 10 kujenga miundombinu ya mawasiliano ya kata hizo,” alisema.Mkataba huo wa TTCL na Huawei ni moja ya juhudi zinazofanywa na kampuni hiyo katika kutekeleza mikakati endelevu ili kuboresha na kupanua upatikanaji wa huduma nafuu za mawasiliano ya simu na intaneti nchi nzima.Aidha Ofisa Mtendaji Mkuu huyo alisema, tangu mwaka jana kampuni hiyo iko katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya mageuzi ya kibiashara, kiufundi, masoko na mauzo ikiwa ni sehemu ya kwanza ambayo inatarajiwa kukamilika mwaka 2017.Alisema miradi hiyo ikikamilika kampuni hiyo itakuwa na mabadiliko makubwa katika utoaji huduma kwa wananchi na itaiwezesha TTCL kutoa huduma bora zaidi za mawasiliano nchini na kwa bei nafuu.Kazaura aliwahakikishia Watanzania kuwa kampuni hiyo ya TTCL iko imara na imejipanga kimkakati kuhakikisha inaendelea kutoa huduma endelevu, bora na nafuu kwa wateja wake wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.Naye Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Bruce Zhang, alisema kwa sababu TTCL ni kampuni kongwe katika huduma za mawasiliano nchini Tanzania, Huawei inatarajia kuwa kupitia kampuni hiyo huduma za simu na mawasiliano kwa ujumla zitasambazwa na kuenea kwa kasi hadi vijijini.
5
Mwandishi Wetu,Dar es Salaam ZAIDI ya wafanyabiashara 2000 katika mkoa wa kodi wa Ilala wamepatiwa elimu ya kodi inayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini.Mamlaka hiyo imekuwa na ikifanya kampeni ya elimu ya kodi mara kwa mara kwa kuwafata wafanyabiashara kwenye biashara zao (mlango kwa mlango). Akizungumzai zoezi hilo Afisa Msimamizi wa Kodi wa mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Zakeo Kowelo alisema kuwa katika siku sita za zoezi hilo, jumla ya wafanyabiashara 2,165 wamepatiwa elimu mbalimbali ya kodi. Alisema maeneo ambayo wamewafikia wafanyabiashara na kuwapatia elimu ni Tabata, Relini, Bima, Liwiti, Barakuda, Kimanga, Segerea, Kinyerezi, Kisiwani na Bonyokwa Mkoa wa Kodi wa Ilala. Alisema zoezi limeenda vizuri na kwamba wafanyabiashara wametoa ushirikiano wa kutosha kwa kutoa taarifa muhimu na kuonyesha nyaraka ambazo zilihitajika jambo ambalo limewawezesha kuwapa ushauri na elimu inayostahili. “Kwa hili tunawashukuru sana kwani tumeweza kuwaelimisha kama tulivyopanga”, alisema KoweloAlisema zoezi lilihusisha kupita duka kwa duka na kuangalia taarifa za wafanyabiashara za kodi ambapo baada ya kuangalia taarifa walifanya majadiliano na kumshauri mfanyabiashara jinsi ya kutunza kumbukumbu. Aliongeza kuwa kwa wale ambao hawajasajili biashara zao wameelekezwa taratibu za kusajili ili watambulike kuwa walipakodi na kwamba pamoja na kusajili biashara pia wafanyabiashara wameshauriwa jinsi ya kujisajili na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na wale wanaostahili kutumia mashine za kodi za kielektroniki wamepewa utaratibu wa kupata na kuzitumia mashine hizo. “TRA ni sehemu ya biashara za wananchi hivyo lengo letu ni kuwaelimisha wananchi ili wafanye biashara kwa usalama zaidi na kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi sahihi na kwa wakati’, alisema Kowelo. Naye Stewart Kimbaga mfanyabiashara wa duka la urembo maeneo ya Bonyokwa alisema kuwa kampeni hiyo ya elimu ya kodi ni nzuri na kwamba itasaidia kutokana na kuwa baadhi ya wafanyabiashara hawana uelewa wa jinsi ya kufanya biashara ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kulipa kodi. Alisema hiyo ni fursa muhimu na kwamba ukaguzi peke yake hautoshi bali unatakiwa uambatane na elimu ili kuwaongezea wananchi uelewa na kujenga uhusiano mzuri baina ya TRA na walipakodi. Zoezi la kutembelea walipakodi katika maeneo yao ya biashara ni mkakati ambao TRA inautekeleza ili kuwaelimisha walipakodi, kuwapa ushauri wa kitaalamu kuhusu taratibu za kulipa kodi, kusajili biashara ambazo hazijasajiliwa, kuwakumbusha kulipa kodi, kutatua changamoto zinazo wakabili na kupata maoni yao kuhusu huduma inayotolewa na TRA kwa ajili ya kuboresha utendaji wake.
5
Ratiba ya hatua ya mtoano ya michuano hiyo inatarajiwa kupangwa leo ambapo itazikutanisha timu zilizotolewa kwenye hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika na zile zilizotinga hatua ya mtoano Kombe la Shirikisho.Yanga ilitolewa na Township Rollers kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa kwa jumla ya mabao 2-1 iliyofungwa nyumbani kabla ya kutoka suluhu Botswana hivyo imejikuta ikiwa ni moja kati ya timu zilizoangukia kwenye michuano hiyo.Akizungumza na waandishi wa habari klabuni Yanga jana, msemaji wa timu hiyo, Dismas Ten, alisema benchi la ufundi limetathmini mchezo uliopita na kujua makosa hivyo wanataka kujipanga vizuri wasiyarudie kwenye michuano hiyo na hatimae wafike mbali.Alisema kuwa lengo lao kwa sasa ni kutaka kuhakikisha inajiandaa mapema kwa kukabiliana na mpinzani wao kwani lengo lao ni kutinga hatua ya makundi na hatimae kusonga mbele zaidi.“Baada ya kumjua mpinzani wetu timu itaanza maandalizi makali kwa ajili ya michuano hii, safari hii hatutaki kurudia makosa, tumeshajirekebisha na tunataka kuona jinsi timu itafanya vizuri kwenye michuano hii.Wakati huohuo, Yanga kwa kushirikiana na kituo cha runinga cha Azam TV kimeandaa kipindi maalumu kwa ajili ya klabu hiyo kitakachojulikana kama Yanga TV Show. Azam imekuwa ikifanya hivyo kwa baadhi ya timu za Ligi Kuu ambapo tayari kuna kipindi cha Azam Tv na Simba Tv.Mkuu wa Kitengo cha Michezo wa Azam Media, Baruani Muhuza, alisema jana kuwa kipindi hicho kitaanza kurushwa mapema mwanzoni mwa mwezi ujao.Alisema kuwa kipindi hicho kitakuwa ni tofauti na vipindi vya timu zilizopita kama Azam na Simba kwani wamejiandaa vizuri. Alisema kuwa utofauti utakaokuwa ni kwamba kitakuwa kikiandaliwa kwa sehemu kubwa na klabu ya Yanga hivyo kutoa fursa ya kuonesha mambo mengi ya klabu hiyo.“Aprili mosi kipindi hicho kitaanza kuruka hewani na kila kitu kinakwenda vizuri, tumeingia mkataba na Yanga na kwa asilimia kubwa kipindi kitakuwa kikiandalia kwenye klabu…“Kutakuwa na wachambuzi ambao ni wataalamu wakiwemo wachezaji wa zamani wa Yanga na hata wa sasa hivyo kitakuwa ni cha utofauti mkubwa zaidi ya vile vya timu zingine,” alisema Muhuza.Mbali na hilo, pia Yanga wameingia mkataba na Kampuni ya Media Solution ambapo itatoa huduma kwa mashabiki na wapezni wa Yanga kupata taarifa kila wakati kupitia simu zao za mkononi.Mmoja wa wawakilishi wa kampuni hiyo, Philemon Kabuje, alisema kuwa shabiki atajiunga na mara moja ataanza kupata taarifa kila mara zinapotokea.“Huduma hii itawawezesha wale wote wanaopenda kupata taarifa za Yanga kuzipata mara moja kila zinapotokea hivyo ni wao kujiunga na huduma hii,” alisema Kabuje. Mahasimu wa Yanga, Simba tayari wameshaingia kwenye mfumo huo tangu mwaka jana ambapo mashabiki wake na wale wa soka hupata taarifa za klabu hiyo kwenye Simba App.
4