text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
JUDITH PETER NA THERESIA GASPER, DAR WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika, Yanga wanakutana na miamba ya soka barani Afrika, Al Ahly kwenye hatua ya 16 bora, huku wakionekana kuwazidi katika idara ya ushambuliaji kutokana na wingi wa mabao Wanajangwani hao waliyonayo. Kwa kulinganisha viwango vya soka vya timu hizo, Al Ahly wamewazidi kwa mbali Yanga kutokana na kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika mara nane huku Yanga wakiwa hawana historia ya kunyakua taji hilo. Yanga wamefanikiwa kuingia raundi ya pili ya Klabu Bingwa Afrika kwa kuiondosha nje ya michuano hiyo, APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2, ikiwa ni ushindi wa 2-1 ugenini na sare ya 1-1 nyumbani. Katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wamecheza michezo 21 sawa na Al Ahly kwenye ligi ya nchini Misri, lakini Wanajangwani hao wanaonekana kuwazidi wapinzani wao kwa kufanya vizuri zaidi. Katika mechi 21 ambazo Yanga wamecheza Ligi Kuu, wamejikusanyia pointi 50 baada ya kushinda mechi 15, kufungwa moja na kupata sare mara tano, tofauti na miamba hiyo ya soka barani Afrika iliyofikisha pointi 47. Al Ahly ambao wanaongoza Ligi Kuu ya nchini Misri kutokana na pointi 47 walizonazo, wamefanikiwa kushinda mechi 14, kufungwa mara mbili na kupata sare mbili huku washambuliaji wake wakitikisa nyavu mara 35 na kuruhusu kufungwa mabao 14. Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi, lakini safu yake ya ushambuliaji inaonekana kuwa imara zaidi kutokana na kutikisa nyavu mara 51 na kukubali kufungwa mabao 11 kwenye ligi hiyo. Rekodi za timu hizo katika Ligi Kuu, zinaonesha kuwa Yanga ndiyo timu pekee iliyoruhusu nyavu zake kutikisika mara chache kutokana na mabao 11 waliyofungwa, huku Al Ahly wakifungwa mabao 14 ambayo ni machache ukilinganisha na timu nyingine katika ligi ya Misri. Kulingana na rekodi za ligi msimu huu, safu ya ushambuliaji ya Yanga inaonekana kuwa imara zaidi kwa kufunga mabao mengi, ambapo mshambuliaji wake, Amissi Tambwe, amefunga mabao 17 huku Donald Ngoma akitikisa nyavu mara 13. Tambwe na Ngoma ndio wanaweza kuwa tishio zaidi kwa Al Ahly wakati wakijiandaa kukutana mwezi ujao, lakini kwa upande wa Wamisri hao wachezaji wanaoweza kuwasumbua Yanga ni kiungo, Abdalla El Saidi na mshambuliaji, Malick Evouna, waliopo katika kinyang’anyiro cha ufungaji bora. Kwa upande wao Azam ambao pia wametinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, watakutana na timu ngumu kutoka nchini Tunisia, Esperance ambao wameshiriki mara nyingi michuano hiyo na kupata mafanikio. Juzi wanalambalamba hao walifanikiwa kuwatupa nje ya michuano ya Kombe la Shirikisho, Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 7-3, ikiwa ni ushindi wa mabao 3-0 ugenini na 4-3 nyumbani. Azam wanashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara, baada ya kuvuna pointi 50 kutokana na michezo 21 waliyocheza, sawa na wapinzani wao Esperance waliojikusanyia pointi 50 baada ya kushuka dimbani mara 19. Rekodi za timu hizo zinalingana hasa katika upande wa ufangaji, ambapo kila timu imetikisa nyavu mara 37, lakini Azam wakiwa wamefungwa mabao 13 na Esperance 15. Juzi mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast, Kipre Tchetche, aliweza kuweka rekodi baada ya kuifungia timu yake ya Azam mabao matatu ‘hat trick’ katika mchezo wa marudiano dhidi ya Bidvest. Kutokana na mafanikio waliyopata Yanga na Azam kwa kuingia hatua ya 16 bora ya michuano ya kimataifa, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amezipa siri ya ushindi inayoweza kuzisaidia kutinga hatua inayofuata ya robo fainali. Akizungumza Dar es Salaam juzi baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Azam na Bidvest Wits uliochezwa katika Uwanja wa Azam Complex, Nape alizitaka timu hizo kutafuta mbinu mpya na kuweka mikakati thabiti ya kuwakabili wapinzani wao. “Nazipongeza Yanga na Azam kwa kufanikiwa kuingia hatua ya 16 bora, lakini sasa wataenda kukutana na Waarabu ambao wapo vizuri kwenye soka, hivyo wanahitaji kufanya mazoezi ya kutosha na kujituma zaidi,” alisema. Alisema kadiri wanavyozidi kusonga mbele watakutana na timu kubwa zenye ushindani na uwezo wa hali ya juu, hivyo ni vyema wakaandaa mikakati itakayowawezesha kufanikiwa na kufika mbali zaidi. | 4 |
Mwandishi Wetu- Dodoma KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Zainab Chaula amewataka watumishi na uongozi wa Hospitali ya Mirembe kuhakikisha wanatembea pamoja kwa kudumisha ushirikiano baina yao ili kuleta mabadiliko chanya, ikiwemo kuboresha huduma zitolewazo na kuboresha stahiki za watumishi katika hospitali hiyo. Dk. Chaula, aliyasema hayo jana alipofanya ziara ya kutembelea Hospitali ya Mirembe na kufanya mazungumzo na watumishi ili kujadiliana namna gani watatatua changamoto walizonazo katika maeneo yao ya kazi. “Tunatakiwa kukaa pamoja na tutembee pamoja wakati wote ili kuleta mabadiliko katika hospitali na taasisi yetu, tuache kulalamika maana sisi sote tulio hapa ndio Serikali yenyewe,” alisema. Aliagiza uongozi wa hospitali hiyo kuwa wabunifu kwa kuhakikisha wanasimamia miradi yao vizuri, hali itakayosaidia kuongeza makusanyo ya mapato na kupelekea kuboresha huduma za afya na stahiki za watumishi katika hospitali hiyo. “Hospitali inatakiwa iwe ya mfano, mnatakiwa kuongeza jitihada na ubunifu katika utendaji wenu, ikiwamo usimamizi mzuri wa miradi, tunataka kuona mabadiliko ili kuweza kusonga mbele,”alisema. Aliagiza maboresho katika maabara, huku akiahidi kurudi baada ya wiki moja ili kuona maboresho yaliyofanywa, ikiwa ni sehemu ya usimamizi na ufuatiliaji wa maboresho ya huduma zinazotolewa katika hospitali hiyo. Aliwataka kujiepusha na vitendo vya rushwa ili kutenda haki kwa kutoa huduma kwa usawa kwa wagonjwa wote maeneo ya kazi. | 0 |
TIMU ya soka ya Yanga jana iliendeleza ushindi ikiwa chini ya kocha wa muda Charles Boniface baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya JKT Tanzania kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.Mkwasa anaifundisha Yanga akichukua mikoba ya Mcongo Papa Mwinyi Zahera aliyetimuliwa hivi karibuni baada ya timu hiyo kusuasua. Kwa matokeo hayo Yanga imrfikisha pointi 13 baada ya kucheza mechi sita baada ya kushinda mechi nne, sare moja na kufungwa moja na kuendelea kuikimbiza Simba inayoongoza ligi hiyo.Hatahivyo, Yanga imecheza mechi chache baada ya kuwa na majukumu ya kimataifa kabla ya kutolewa katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika. Katika mchezo wa jana, Yanga walipata bao lao la kwanza kupitia kwa Patrick Sibomana baada ya kupata pasi kutoka kwa Deus Kaseke, lakini furaja zao hazikufumu sana kwani JKT Tanzania walisawazisha dakika mbili baadae kwa baio la Adam Adam.Adam alifunga bao hilio baada ya kupata pasi kutoka kwa Farouk Shikalo aliyefanyakazi nzuri kabla ya mfungaji hajaujaza mpira wavuni. Yanga waliandika nao la pili lililofungwa na Juma Balinya akiunganisha wavuni mpira wa Kaseke.David Molinga aliiandikia Yanga bao la tatu na kuihakikishia timu hiyo kutoka na pointi zote tatu baada ya kufunga bao la tatu katika dakika ya 34 kwa mpira wa adhabu ndogo baada ya Kaseke kuangushwa nje ya eneo la hatari.Dakika ya 45 Molinga nusura aifungie Yanga bao la nne baada ya kupiga mpira wa kichwa, ambao haukulenga lango. Simba wenyewe watashuka dimbani kesho Jumapili kucheza Ruvu Shooting katika muendelezo wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.Kikosi cha Yanga kilichoanza: Farouk Shikalo, Juma Abdul, Jafar Mohamed, Lamine Moro, Ally Mtoni, Papy Tshishimbi, Deud Kaseke, Mapinduzi Balama, David Molinga na Patridc Sibomana. JKT Tanzania: Abdulahaman Mohamed, Michael Aidan, Adeyum Ahmed, Frank Nchimbi, Damas Makwaya, Jabir Stima, Mwinyi kazimoto,. Richard Maranya, Daniel Lyanga, Adam Adam na Edward Songo. | 4 |
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amewataka wazazi na walezi wilayani Karatu kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule hata kama hawana sare za shule.Aidha ameagiza uongozi wa serikali ya kijiji cha Lositete kuchukuliwa maelezo na polisi kuhusu sababu za kutochangia maendeleo ya elimu, badala yake wanaingiza siasa na kusababisha saruji kuganda.Gambo alitoa agizo hilo jana katika kijiji cha Lositete, kata ya Mbulumbulu wilayani Karatu alipokwenda kukagua hali halisi ya madarasa pamoja na idadi ya wanafunzi walioanza masomo ya kidato cha kwanza.Alitoa agizo hilo jana kutokana na taarifa ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Upper Kitete, Josephat Mau iliyodai kuwa wanafunzi tisa kati ya 171 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza shuleni hapo wameripoti shule. Mwalimu Mau alisema wanafunzi hao 162 hawajaripoti shuleni hapo kutokana na kukosekana na sare za shule huku walioripoti wakiwa ni tisa kwa sababu ya wazazi au walezi wao kutouza maharage kwani hakuna soko.Baada ya mwalimu huyo kutoa taarifa hiyo, Gambo aliagiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza kuripoti shuleni na nguo za nyumbani hata kama hawana sare ili waendelee na masomo wakati wazazi wao wakisubiri kuwanunnulia mahitaji ya shule. “Rais ameagiza elimu bure hivyo wazazi au walezi watoeni watoto wenu majumbani ili waende shule bila ya kuwa na sare za shule huku mkiendelea kutafuta sare lakini pia nasisitiza nyie wananchi acheni kuingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo, “alisema.Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Lositete na Upper Kitete, Gambo aliagiza mwenyekiti wa kijiji cha Upper Kitete, William Safari pamoja kuhakikisha wanasoma mapato na matumizi ya kijiji ambayo wananchi wanadai hawajasomewa tangu mwaka 2017 hadi mwaka jana. Awali, baadhi ya wananchi walidai kuwa wameshindwa kujenga madarasa pamoja na maabara kwa sababu walichanga fedha ambazo inadaiwa zililiwa na aliyekuwa mkuu wa shule hiyo, Andrew Sulle. Anadaiwa kuchukua Sh milioni nane.Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Theresia Mahongo alisema wananchi zaidi wa vijiji vya Lositete na Upper Kitete wanapenda kuingiza masuala ya siasa katika maendeleo. Alisema amejitahidi kutatua changamoto zao ikiwamo kuhakikisha mwalimu huyo anachukuliwa hatua za kinidhamu na ameshahukumiwa kifungo. Alisema wanafunzi 5,313 walifanya mtihani wa darasa la saba mwaka jana huku wanafunzi 4,000 sawa na asilimia 75.3 walifaulu.Wanafunzi 3,446 wamepangwa kwenye shule za kata zilizokuwa na madarasa 83 na wanafunzi 539 walikosa nafasi. Alisisitiza kuwa wanafunzi hao 539 waliokosa nafasi hivi sasa wameshaanza masomo katika shule mbalimbali za wilaya hiyo kutokana na kubainika kuwapo shule ambazo wanafunzi hawakupangwa. Alisema wanaandika barua kwa wadau na kuhamasisha wanananchi kujenga madarasa pamoja na kukarabati viti na meza ili wanafunzi waweze kusoma. | 3 |
LEO ni siku ya mwisho ya matumizi ya mifuko ya plastiki hapa nchini, kwa kuwa operesheni ya kitaifa ya kuiondoa mifuko hiyo inaanza rasmi kesho.Katika operesheni hiyo, serikali imeainisha mifuko na vifungashio vya plastiki vilivyopigwa marufuku na vile vilivyoruhusiwa katika operesheni ya kuondoa mifuko hiyo, inayoanza kesho nchi nzima.Serikali imesema katika operesheni hiyo, ukaguzi utafanyika madukani, magengeni, masokoni, kwenye maduka makubwa (supermarkets), ghalani, mipakani, viwandani na kwenye maeneo mengine zinakouzwa bidhaa. Katazo hilo linatokana na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Sura 191 pamoja na Kanuni za Usimamizi wa Mazingira za Kupiga Marufuku Mifuko ya Plastiki za Mwaka 2019.Mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku hii hapa Mwanasheria wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Manchare Heche, alisema jana mifuko iliyopigwa marufuku ni mifuko yote ya plastiki inayotumika kama vibebeo.Alisema mifuko hiyo hutumiwa na wananchi wengi, kubebea bidhaa wanapokwenda sokoni, madukani au magengeni au ile ambayo wauzaji wa bidhaa, huitumia kuwahifadhia wateja wao bidhaa.Kwa mujibu wa Heche, mifuko hiyo inakatazwa kuzalishwa, kusambazwa, kuuzwa, kuhifadhiwa na kutumiwa na mtu yeyote na atakayekwenda kinyume na katazo hilo, atakuwa ametenda kosa na atastahili adhabu kwa mujibu wa sheria.Mbali na vibebeo hivyo vya mifuko ya plastiki, Mwanasheria huyo wa NEMC alisema hata vifungashio vya mifuko ya plastiki vinavyotumika kufungashia maji ya kunywa maarufu Kandoro, karanga na barafu navyo vimepigwa marufuku.Vifungashio vingine alivyovitaja ambavyo vimepigwa marufuku ni mifuko ya plastiki ya kufungashia sabuni za unga na binzari, kwa kuwa ni laini na ina athari kwa mazingira na viumbe hai.Adhabu kwa watakaokutwa na mifuko hii Watu watakaokaidi katazo la mifuko ya plastiki, watakabiliwa na adhabu mbalimbali kulingana na kosa la mhusika. Akizitaja adhabu hizo, Heche alisema watumiaji ambao wengi ni wananchi wa kawaida adhabu yao ni faini ya Sh 30,000 hadi Sh 200,000 au kifungo cha siku saba au vyote kwa pamoja. Kwa wauzaji wadogo, wao watakabiliwa na adhabu ya faini ya Sh 100,000 hadi Sh 500,000 au kifungo cha miezi mitatu au vyote kwa pamoja.Adhabu nyingine ni faini ya Sh milioni 5 hadi Sh milioni 20 kwa mtu atakayekamatwa kusafirisha mifuko hiyo nje ya nchi au kifungo cha miaka miwili au zote mbili kwa pamo; faini ya Sh milioni 5 hadi Sh milioni 50 kwa mtu atakayebainika kuhifadhi au kusambaza mifuko ya plastiki au kifungo cha miaka miwili au vyote kwa pamoja.Mtu atakayebainika kuzalisha au kuingiza nchini mifuko na vifungashio vya plastiki vilivyokatazwa, atakabiliwa na adhabu ya kulipa faini kati ya Sh milioni 20 hadi Sh bilioni 1 au kifungo cha miaka miwili jela au adhabu zote mbili kwa pamoja.Mifuko ya plastiki iliyoruhusiwa kwa masharti makaliKwa mujibu wa Heche, baadhi ya mifuko na vifungashio vya plastiki vimeruhusiwa, kwa kuwa vimekidhi viwango katika uhifadhi wa mazingira.Aliitaja mifuko iliyoruhusiwa kuwa ni ile ya kuhifadhia taka katika maduka makubwa, hospitali, shule, maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu, mifuko inayotumika kwenye shughuli za ujenzi. Vifungashio vilivyoruhusiwa ni vile vinayotumika kwenye sekta ya kilimo kwa ajili ya kuoteshea mbegu au miche, vifungashio kwa ajili ya vyakula kwa ajili ya kuhifadhia ubora wa chakula kama vile korosho, mikate, mchele, sukari ambavyo vinakubalika kisheria.Katika kuhakikisha vifungashio visivyoruhusiwa havipati nafasi tena kwa watumiaji, Heche alisema kazi ya kuvipiga marufuku imeanzia kwenye viwanda vinakozalishwa na kwa wauzaji wakubwa, hivyo vitatoweka kupitia operesheni hiyo.Hata hivyo, watumiaji wa aina hii ya mifuko na vifungashio, wana wajibu wa kuhakikisha taka zitokanazo na mifuko au vifungashio hivyo, zinasimamiwa kwa mujibu wa Kanuni za Usimamizi wa Taka Ngumu na Kanuni za Usimamizi wa Taka Hatarishi za Mwaka 2009, ambapo watakaokiuka watakabiliana na adhabu kali zaidi. Mathalani, endapo mtu atatumia aina hii ya mifuko ya plastiki iliyoruhusiwa, lakini akashindwa kutunza vizuri baada ya matumizi kwa mfano akatupa hovyo pakiti ya maziwa baada ya kunywa, au akatupa hovyo kifungashio cha mkate au korosho, atakumbana na faini kali ya Sh 200,000 kwa mtu binafsi na kama ni kampuni adhabu yake ni Sh milioni 5.Kondomu ni plastiki au si plastiki?Kwa kuwa mipira ya kiume ijulikanayo ni sehemu ya plastiki zisizooza kwa urahisi, Heche alisema japo mipira hiyo ina sifa zote mbili ya kuwa kibebeo na kifungashio, haitahusika kwenye operesheni hiyo. Alisema kondomu zinaangukia kwenye kundi la vibebeo au vifungashio vya afya, hivyo haijapigwa marufuku na sheria inayokataza mifuko ya plastiki, kwa vile matumizi yake yanazingatia matakwa ya kiafya.Uzalishaji, matumizi mifuko ya plastiki Kwa mujibu wa Ofisa Mazingira Mwandamizi wa NEMC, Ndimbumi Joram, tani milioni 300 za mifuko ya plastiki, huzalishwa kila mwaka duniani kote wakati kwa Tanzania tani 24,000 huzalishwa kila mwaka kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2016. Ndimbumi alisema mifuko ya plastiki trilioni tano, hutumika kila mwaka duniani kote.Alisema kiwango hicho ni sawa na wastani wa mifuko 160,000 kutumika kwa sekunde na kwa wastani mtu mmoja hutumia mifuko 700 ya plastiki kwa mwaka. Mwanasheria wa NEMC alisema awali kuwa asilimia moja tu ya mifuko yote inayozalishwa hapa nchini, ndiyo inachakatwa, ikilinganishwa na Marekani inayochakata asilimia 23 ya mifuko hiyo. Mifuko ya plastiki huchukua miaka 500 hadi 1,000 kuoza. | 3 |
NA HADIA KHAMIS
MSANII mwenye jina kubwa katika muziki wa Bongo Fleva nchini, Juma Kassim Kiroboto ‘Juma Nature’, anatarajia kusherehekea miaka 16 ya mafanikio yake hivi karibuni.
Mafanikio hayo atayafurahia katika tamasha la Komaa Concert ambapo watashirikiana na kituo cha Redio cha EFM kinachosherehekea mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Mkurugenzi wa mawasiliano wa kituo hicho, Dennis Sebbo, alisema tamasha hilo litafanyika katika Manispaa ya Temeke ikiwa ni heshima ya msanii huyo kwa kuzaliwa huko na ni wilaya ambayo kitio hicho kilianzishwa kwa mara ya kwanza.
Nature alisema ataadhimisha kwa kutembelea wagonjwa katika Hospitali ya Temeke ambapo atatoa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa kisha jioni yake ataendeleza onyesho kabambe.
“Miaka 16 ni mingi katika sanaa ukizingatia enzi hizo tunaanza kazi katika sanaa tulikuwa tunatembea kwa miguu kutoka Kurasini hadi kwa Master J, Masaki kwa ajili ya kurekodi na wakati mwingine haupati nafasi hivyo tunatakiwa tumshukuru Mungu kwa hali ilivyo sasa,” alisema Nature. | 1 |
['Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amefutilia mbali uwezekano wa kumsajili kiungo wa kati wa Barcelona, Philippe Coutinho, 27, ambaye aliondoka Anfield kwa kima cha £142m mwaka 2018. (ESPN)', 'Paris St-Germain imekubali kulipa £28m kumsajili kiungo wa kimataifa wa Senegal Idrissa Gueye, 29, kutoka Everton. (Mail)', 'Toffees wanaendelea kushauriana na Crystal Palace kuhusu usajili wa nyota wa kimataifa wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, kwa pauni £80m. (Sky Sports)', 'Tottenham imewasiliana na Juventus kuhusu usajili wa nyota wa kimataifa wa Argentina international mshambuliaji Paulo Dybala, 25, ambaye bei yake anayekadiriwa kuwa £80m. (Evening Standard)', 'Manchester United wameomba kufahamishwa kuhusu hatma ya mchezaji Christian Eriksen, 27, wa Tottenham. Kandarasi ya nyota huyo wa kimataifa wa Denmark amesalia na mwaka mmoja kukamilika na huenda akauzwa kwa pauni milioni 70. (Mail)', 'United pia inamlenga mshambuliaji wa Lille na nyota wa kimataifa wa Ivory Coast Nicolas Pepe, 24, ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa £70m, kuchukua nafasi ya mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku endapo atajiunga na Inter Milan. (Times)', 'Kiungo wa kati wa Kimataifa wa Serbia na Lazio Sergej Milinkovic-Savic, 24, amewaambia wachezaji wenzake kuwa ataondoka klabu hiyo msimu huu licha ya tetesi huendaakajiunga na Manchester United. (Il Tempo via Express)', 'Chelsea na West Ham wanapania kumsajili kwa mkopo winga wa Portsmouth Leon Maloney, 18 ambaye ameifungia Pompey academy mabao 26 msimu uliopita. (Sun)', 'Wolfsburg na RB Leipzig wanataka kumsajili kwa mkopo winga wa Arsenal wa miaka 18 Muingereza Emile Smith Rowe. (Independent)', 'Crystal Palace na Aston Villa wanataka kumsajili kiungo wa kimataifa wa Jamhuri ya Ireland anayecheza safu ya mashambulizi Jonathan Afolabi ambaye aliondoka Southampton mwisho wa msimu uliopita. (Football.London)', 'Sheffield United ambao wamepandishwa daraja kushiriki ligi kuu ya Premia wanatafakari uwezekano wa kumnunua kipa wa zamani wa kimataifa wa England Joe Hart, 32, kutoka Burnley. (Mail)', 'Villa wanashauriana na kipa wa Juventus, Mtaliano Mattia Perin baada ya uhamisho wake £13m kwenda Benfica kugonga mwamba baada ya kukosa uchunguzi wa kiafya. (Football Italia)', 'Barcelona wameweka dau la £24m kumnunua mlinzi wa Real Betis na Uhispania Junior Firpo. (Sport - in Spanish)', 'Tetesi Bora Jumatano', "Paris St-Germain wameishinda Juventus katika kinyang'anyiro cha kumsaini mlinzi wa Tottenham Danny Rose, 29, na wanaamini watafikia mkataba wa pauni milioni 20 kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa England . (Sun)", 'Naibu mwenyekiti mkuu wa Manchester United, Ed Woodward yuko mbioni kushughulikia suala la usajili wa wachezaji wapya, zikiwa zimesalia wiki mbili kabla ya muda wa mwisho wa uhamisho wa wachezaji kukamilia. (ESPN)', 'Woodward ana matumaini ya kukamilisha mchakato wa usajili wa mlinzi wa timu ya taifa ya England na klabu ya Leicester City, Harry Maguire, 26, na mchezaji wa safu ya kati wa Newcastle Sean Longstaff, 21. (London Evening Standard)', 'Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp bado anapania kumnunua mchezaji mwingine mmoja msimu huu. (Liverpool Echo)', 'Mchezaji wa safu ya kati wa Sporting Lisbon na Ureno Bruno Fernandes, 24, amesema kuwa ataendelea kucheza katika ligi kuu ya Ureno licha ya tetesi zinazomhusisha na uhamisho wa kwenda Manchester United. (Mirror)', 'Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery ana wiki mbili kuamua ikiwa atamuachilia winga wa England wa chini ya miaka-21 Reiss Nelson, 19, kujiunga na Hertha Berlin kwa mkopo msimu ujao. (Sun', 'Tottenham wanakaribia kumsaini kiungo wa kati wa Real Betis Muargentina Giovani lo Celso, 23, kwa kima cha pauni milioni 45. (Sun)'] | 4 |
Kauli hiyo ya Serikali ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa anafungua mkutano wa kila mwaka wa wadau wa korosho uliofanyika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Mipango, mjini Dodoma.Alisema nia ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha vikwazo vyote vilivyokuwa vinawakabili wakulima wa zao hilo vinaondolewa ili kuwawezesha kupata tija zaidi kutokana na zao lao.“Mheshimiwa waziri wa kilimo mifugo na uvuvi, hebu sema lile tuliloazimia kuhusu pembejeo kuanzia msimu wa mwaka huu… tunataka wajumbe wa mkutano huu muhimu wajue nini sisi kama serikali tumekubaliana”, alisema Majaliwa huku akimwinua waziri huyo kutoa kauli ya serikali kwa niaba yake.Alisema lengo la Serikali ni kuona mashamba yaliyotelekezwa na yenye mikorosho iliyozeeka yanafufuliwa ili kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa wakulima na nchi kujipatia kipato cha kutosha.“Mikorosho asilimia 25 iliyopo sasa ni ile iliyozeeka ambayo haizalishi kiasi cha kuridhisha…lakini pia kuna mashamba yaliyotelekezwa kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukosa mitaji kwa ajili ya kununua pembejeo,hivyo basi kwa hatua hii tunatarajia yatafufuliwa”, alisema Majaliwa huku akishangiliwa na wadau hao.Awali akitoa taarifa kwa mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Nchini (CBT), Anna Abdallah, alisema bodi hiyo imenunua tani 18,000 za pembejeo aina ya Salfa ambayo inatumika kudhibiti na kutibu ugonjwa wa ubwiriunga unaowasumbua wakulima wa zao hilo.Alisema kiasi hicho ni sawa na asilimia 95 ya pembejeo zote zilizoagizwa kwa msimu huu wa kilimo, ambapo pembejeo nyingine ni pamoja na dawa za maji za kunyunyizia na mabomba ya kupulizia na jumla ya Sh bilioni 43.5 zitatumika katika kununua, kusambaza na malipo ya mawakala.“Mwaka huu tutafikisha pembejeo za ruzuku hadi wilayani badala ya ule mfumo wa miaka yote wa kuwa na vituo vichache…na tayari tumeshapokea pembejeo zote tunasubiri muda muafaka tuanze kusambaza kwa wakulima,” alisema Anna.Akitoa taarifa za mapato yatokanayo na mazao ya biashara, Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Ushirika, Dk Charles Tizeba alisema korosho imeongoza kwa kuliingizia taifa fedha za kigeni kutokana na mauzo ya zao hilo nje ya nchi katika msimu uliopita.Tizeba alisema jumla ya dola za kimarekani milioni 300.46 (sh bilioni 630.9)n zilipatikana kutokana na mauzo hayo na hivyo kuongoza na kufuatiwa na zao la tumbaku, katika msimu huo tani 260,000 zilikusanywa na kuuzwa kwa mnada kwa wanunuzi wa ndani na nje ya nchi.Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa amewaonya watendaji wa serikali na viongozi wa vyama vya ushirika wanaoshirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kununua korosho nje ya mfumo wa ununuzi wa stakabadhi ghalani (kangomba) na kwamba ikibainika watachukuliwa hatua kali za kisheria.Alisema serikali kuanzia msimu uliopita imefanya mazungumzo na wanunuzi wakubwa kutoka nchi mbalimbali ili kuja nchini kununua korosho badala ya kutegemea wafanyabiashara kutoka India pekee kama ilivyozoeleka na matokeo ni kupanda kwa bei ambapo ilifikia hadi Sh 4,000 kwa kilo. | 5 |
Ramadhan Hassan -Dodoma WABUNGE wametaka wachezaji wa
kulipwa wanaonza kikosi cha kwanza kutozidi wanne, ili kuwapa nafasi wachezaji
wazawa. Wakichangia jana bungeni
bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo kwa mwaka 2020-2021,wabunge
hao walidai kwamba wachezaji wa kulipwa wanaotoka nje ya nchi wamekuwa wengi
hivyo kuna haja ya Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) kuliangalia kwa umakini jambo
hilo. Mbunge wa Kilolo,Venance
Mwamoto(CCM), alisema TFF inatakiwa kuweka utaratibu wachezaji wa kulipwa
wanaonza kikosi cha kwanza kutozidi wanne ili kuwapa nafasi wachezaji wazawa. “Wachezaji wanatoka nje ya
Tanzania kwa sasa wapo wengi lakini suala la wanaotakiwa kuanza katika kikosi
cha kwanza ni vizuri ukawekwa utaratibu mzuri zaidi na mimi nashauri wawe wasizidi
wanne,”alisema. Alitolea mfano wa timu ya
Taifa ya Uingereza kwa kusemna kutofanya kwake vizuri katika michuano
mbalimbali kutokana ligi za nchi hiyo kujaza wachezaji wengi wa kulipwa hivyo ni
vizuri TFF ikaliangalia jambo hilo. Mwamoto pia aliishauriTFF
kurudisha mashindano ya Taifa akisema wakati yanafanyika yaliibua vipaji vya
wachezaji wengi. “TFF waje kwetu wabunge tuwape
maoni jinsi ya kuendesha soka la Tanzania,”alisema Mwamoto. Mbunge wa Mufinga Mjini, Cosato
Chumi (CCM), alisema malalamiko ya waamuzi kuchezesha chini ya kiwango yamekuwa
mengi hivyo kuna haja ya TFF kuliangalia jambo hilo kwa umakini. “Bila kuwa na waamuzi bora
hatuwezi kuwa na ligi bora hivyo jambo hili tunaomba liangaliwe kwa umakini,”alisema
Chumi. | 4 |
JUMLA ya tani 160 za korosho zenye thamani ya Sh milioni 550, zimenunuliwa kutoka kwa wakulima wilayani Tunduru mkoani Ruvuma katika kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kutaka serikali kununua korosho hizo kutokana na wanunuzi kulegalega.Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania(TADB) imetoa fedha hizo kwa wakulima 534 wa wilaya hiyo, ikiwa ni sehemu ya malipo ya korosho zao kwa msimu huu wa mwaka na tayari zimeshaanza kuchukuliwa na malori ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya kubanguliwa.Akizungumza wakati wa ubebaji wa korosho hizo, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera alisema jumla ya malori 10 ya jeshi yameshawasili kwa ajili ya kubeba korosho ambazo zimeshanunuliwa na serikali kupitia Benki ya TADB.“TADB imefanya uratibu mzuri kuhakikisha kila mkulima anapata fedha yake kulingana na mzigo wake na bei ya korosho iliyopangwa ya shilingi 3,300 kwa kilo. Tunashukuru zoezi hili limekwisha salama na sasa tunapakia,” alisema Homera.Alisema wakulima wa korosho katika wilaya yake, walionesha kukata tamaa baada ya kukosa wanunuzi kwa bei ya kuanzia Sh 3,000 hivyo kwa hatua zilizochukuliwa na serikali imewapa nguvu na kuendelea na kilimo cha zao hilo baada ya kununua kwa Sh 3,300 kwa kilo moja.“Wakulima kuwepo katika vyama vya ushirika imesaidia kuwa na msimamo na kuondoa adha ya wakulima kuuza korosho holela kwa waranguzi kwa kukosa fedha za kujikumu baada ya kukosa soko la mazao yao,” alisema Homera.Mkuu wa Wilaya huyo alisema TADB haikupata shida katika kuratibu kazi ya ulipaji fedha kwa wakulima kutokana na uwepo wa vyama vya ushirika wilayani humo ambavyo vimesaidia kufanya utambuzi wa kila mkulima na idadi ya zao lake.“Kazi hii limepelekea vijana kupata ajira ya kupakia korosho kwenye malori na zaidi kupelekea mzunguko wa fedha wilayani kuongeza kwa wakulima kulipwa fedha zao,” alisema Homera.Meneja wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) wilayani Tunduru, Shauri Mokiwa aliwataka wakulima watumie fedha walizozipata kununua viutatilifu mapema ili kipindi cha kupiga dawa kitakapofika wasipate tabu. “Pembejeo tunazo za kutosha kwa msimu ujao hivyo ni uamuzi wao wakulima kuja kununua ili waweze kuboresha ubora wa korosho kwa msimu ujao.”alisema. | 3 |
NA WAANDISHI WETU-DAR/MWANZA RAIS Dk. John Magufuli, amepindua hoja ya kuvunjwa kwa Katiba baada ya kumteua Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Dk. Abdallah Possi kuwa balozi. Uamuzi huo wa Rais Magufuli, umekuja huku kukiwa na mjadala mpana wa kudaiwa kuvunja Katiba kwa kuminya nafasi za uteuzi za wabunge wanawake. Taarifa iliyotolewa jana usiku na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu wakati tunakwenda mitamboni, ilieleza kuwa kituo cha kazi na tarehe ya kuapishwa kwa balozi huyo mteule vitatangazwa baadaye. Kabla ya uteuzi huo, Dk. Possi alikuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu aliyekuwa akishughulikia walemavu. Kutokana na uteuzi huo, nafasi yake itajazwa baadaye. Inaelezwa kuwa kutokana na uteuzi huo wa Dk. Possi, kuna hatari katika Bunge lijalo linaloanza vikao vyake Januari 31, huenda akajiuzulu ubunge ili kutoa nafasi ya uteuzi kwa mtu mwingine. Ikiwa atafanya hivyo, wabunge wa kuteuliwa na Rais watabaki saba, wakiwamo wanawake wawili na wanaume watano. Kwa hesabu hiyo, Rais Magufuli atabakiwa na nafasi tatu za uteuzi wa wabunge kutokana na nafasi 10 alizopewa kwa mujibu wa katiba. | 3 |
JUMLA ya makontena 34 yenye seti za meza na viti 22,000 vimewasili bandarini Zanzibar na vinatarajiwa kuanza kusambazwa katika shule za Unguja na Pemba.Mwenyekiti wa kamati ya madawati kitaifa, Waziri Haroun Ali Suleiman amesema madawati hayo yamewasili kutoka China ambapo yametengenezwa na Kampuni ya Guangzhou Everprety Furniture Limited.Amesema kamati hiyo ilipewa jukumu la kuchangisha wadau mbalimbali madawati kwa ajili ya matumizi ya shule za Unguja na Pemba ambazo zinakabiliwa na tatizo hilo.Amesema jumla ya Sh bilioni 3.8 zimetumika kwa ajili ya kutengeneza samani hizo ambapo kabla kumefanya wanafunzi wengi kusoma sakafuni.''Tumepokea shehena ya makontena yenye seti za samani ikiwemo madawati kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambao wanakabiliwa na tatizo hilo kiasi cha kusoma na kukaa chini,''amesema.Amesema kiasi hicho cha madawati kwa kiasi kikubwa kitapunguza tatizo hilo ambalo limeongezeka kutokana na serikali kutangaza elimu ya maandalizi kuwa ya lazima.Alifahamisha kwamba hiyo ni awamu ya kwanza ya madawati, ambapo awamu ya pili inatarajiwa kuwasili nchini mwezi ujao.Mapema Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Riziki Pembe Juma alisema wizara itahakikisha madawati hayo yanatunzwa huku walimu wakuu wote wakitakiwa kuwa wasimamizi wakuu.Alisema juhudi zaidi zinahitajika katika kutafuta madawati ambapo upo upungufu wa madawati 17,950.''Licha ya kupata kiwango kikubwa cha madawati bado tunakabiliwa na uhaba wa madawati yapatayo 17,950 kwa shule za Unguja na Pemba,'' amesema.Mwaka 2017 Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein aliunda kamati ya watu 11 wakiwemo wafanyabiashara wakubwa kwa ajili ya kulipatia ufumbuzi tatizo la uhaba wa madawati kwa shule za Unguja na Pemba. | 3 |
JAKARTA, INDONESIA MWANAUME mmoja nchini Indonesia aliyeweka sheria dhidi ya uzinzi naye
ameshikwa na kosa la kutembea na mke wa mtu. Mukhlis bin Muhammad kutoka baraza la Aceh Ulema amekuwa kiongozi wa
kwanza kupigwa viboko 28 kwa kosa la uzinzi mbele ya kadamnasi. Mwanamke ambaye alikuwa na mahusiano naye alichapwa viboko 23. Mukhlis anatokea katika mji pekee nchini Indonesia ambao unafuata
sheria za kiislamu , zinazojulikana kama sharia. Mbali na sheria hizo kuwaadhibu wazinzi, pia wanaojihusisha na
mapenzi ya jinsia moja wanaadhibiwa katika umati wa watu kwa kupigwa viboko. Husaini Wahab ambaye ni Meya msaidizi wa eneo hilo la Aceh Besar
aliiambia BBC kuwa; “Hii ni sheria ya Mungu. Mtu yeyote anayekosea lazima
aadhibiwe na sheria hizo,” Wapenzi hao walikamatwa na maofisa mwezi Septemba mwaka huu wakiwa
katika gari ambalo lilikuwa limeegeshwa karibu na ufukwe wa kitalii. Husaini alisema kuwa wapenzi hao walichapwa siku ya alhamisi wiki
hii. Mwanaume huyo aliyekamatwa ugoni ni kiongozi pia wa dini ya ya
kiislamu. Yeye ni kiongozi wa kwanza kupigwa katika kadamnasi kwa mujibu wa
sharia iliyowekwa katika mji huo na kuanza kufanya kazi tangu mwaka 2005. Ofisa huyo ameshauri serikali ya mtaa na watunzi wa sheria ambao
wanatekeleza sheria hiyo kufanya mabadiliko. Aceh ilianzisha sheria ngumu za Kiislamu kwa zaidi ya muongo mmoja
ili watu wapate haki zao. Sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ilianzishwa mwaka 2014 na
kuanza kufanya kazi mwaka uliofuata. Kuwa na wapenzi wengi, kucheza kamali na matumizi ya pombe ni kinyume
na sheria katika sharia ya kiislamu. Mwaka 2017, wanaume wawili walipigwa fimbo 83 huko Aceh baada ya
kukutwa wakifanya mapenzi. | 2 |
KINASHASA, DRC SHIRIKA la Umoja wa Mataifa linalowahudumia watoto, Unicef likishirikiana na washirika wao limetangaza orodha ya watoto 155 ambao wamepoteza wazazi wao au waliachwa bila mlezi kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola uliotokea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Katika taarifa iliyotolewa na shirika hilo nchini humo, Unicef inasema idadi hii inawajumlisha watoto ambao wamepoteza mzazi mmoja, wawili au wanaowatunza ambao walifariki dunia kutokana na Ebola pamoja na wale ambao waliachwa bila mlezi baada ya wazazi wao kutengwa na kuwekwa katika vituo vya matibabu. Taarifa inaendelea kusema kuwa watoto ambao hupoteza wazazi wao kutokana na Ebola wanapata machungu mengi moyoni kwani hunyanyapaliwa, hutengwa na pia hushuhudia mzazi wake au mlezi wake akifariki dunia na hilo ndilo jambo linalowasumbua. Mwakilishi wa Unicef nchini DRC, Dk. Gianfranco Rotigliano, anasema kumpoteza mzazi au mtu wa karibu inaweza kuwa hali ngumu kwa mtoto na jukumu lao kama Unicef ni kuwalinda na vile vile kusaidia watoto wote ambao wameathirika na virusi vya Ebola. Wakati huo huo, Shirika la Afya Duniani (WHO), limetoa idadi mpya ya waliofariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola nchini DRC tokea mwezi Agosti. Msemaji wa WHO, Fadela Chaib, akiwa mjini Geneva Uswisi Ijumaa, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi Septemba 18, idadi kamili ya visa vya Ebola vilivyoripotiwa ilikuwa 143, huku 112 vikibainishwa kuwa Ebola ambapo watu 91 wamepoteza maisha. | 2 |
TANZANIA inaongoza kwa kuwa na tozo zenye gharama nafuu kwenye matumizi ya data pamoja na maudhui katika Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), imeelezwa.Hali hiyo inatokana na uwepo wa Mkongo wa Taifa ambao umesaidia kupunguza gharama za mawasiliano ambapo kwa sasa watumiaji wa data hutozwa Sh 10 kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine. Hayo yalibainishwa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Atashasta Nditiye wakati akifungua Mkutano wa Kimataifa uliokutanisha Mamlaka za Udhibiti wa Mawasiliano (CRASA).Nditiye alisema katika nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na SADC, Tanzania ndio huduma zake za data zipo chini. “Mkongo wa Taifa ambao upo karibu mikoa yote ndio umesaidia kupunguza gharama na nchi kutoka nje wamekuwa wakija kujifunza namna ya uendeshaji wake,” alisema Nditiye. Aliongeza kuwa wananchi wanaweza kuwasiliana kwa gharama nafuu na kwamba malipo wanayoyafanya ni kwa ajili ya kuchangia katika uwekezaji uliofanyika. Pia alisema gharama wanazotozwa waendeshaji wa maudhui na blogs zipo chini na kwamba zinaendana na usalama wa Watanzania. “Gharama tunazotoza ni kwa sababu tunahitaji watu wasivuruge maadili ya Tanzania bali wajifunze matumizi bora ya mawasiliano,” alisisitiza.Naibu Waziri huyo alisema wanashirikiana na jumuiya hiyo katika masuala ya uhalifu wa mtandao, utangazaji wa luninga na redio na kuhakikisha tozo za mawasiliano zinakuwa nafuu ili wananchi wanufaike. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), James Kilaba alisema wamekutana kwa lengo la kupitia changamoto na maendeleo ya mawasiliano katika jumuiya hiyo.Kilaba alisema malengo ya mkutano huo, pamoja na mambo mengine watajadiliana namna ya kuweka uwiano katika tozo na kushughulikia masuala ya mawasiliano kwa ujumla. “Tunataka kuwa na nchi ya viwanda, hivyo ni lazima mawasiliano ya Tehama yawepo na yawe salama kuanzia miundombinu, mitandao na watumiaji,” alisema Kilaba.Aliongeza kuwa kwa kuhakikisha usalama wa mitandao na watumiaji wanahakikisha kuwa wanawatambua watumiaji wote wa simu kwa kuwasajili. Kilaba alieleza kuwa si rahisi kwa jumuiya hiyo kuwa na kanuni moja ya kudhibiti mawasiliano badala yake wanaweka miongozo ambayo kila nchi wanachama wanapaswa kuifuata.“Bado kuna changamoto ya elimu kwa watumiaji wa mawasiliano nchini kwani wengi hawajui namna ya kutumia simu zao hivyo hujikuta wakiingia kwenye matumizi mabaya kwa kutuma picha au video zisizofaa bila wenyewe kujua. Hivyo, tunaomba kila mtu ajue matumizi ya simu kabla ya kuanzia kutumia hii itasaidia kupunguza makosa,” alifafanua. | 3 |
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amekaribisha waliokuwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwamo aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT), Sophia Simba kujiunga na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), aliyasema hayo jana katika taarifa yake.
Alisema wanachama hao walikuwa mashujaa wa kutetea haki, demokrasia na taratibu kwa kupinga dhuluma ndani ya chama chao cha CCM.
“Nafsi yangu imenisukuma kushika kalamu na kuandika haya kutokana na kile kilichotokea Dodoma katika vikao vya CCM.
“Ni takriban miezi 20 sasa toka nilipojitoa CCM, lakini nasikia bado naendelea kutajwatajwa huko katika vikao vyao.
“Wamewatimua wanachama na viongozi wao ambao wengi wao walitumia demokasia yao kupinga upindishwaji wa kanuni na sheria za chama chao.
“Nataka kuwaambia kuwa wakati wakifanya hivyo walikuwa mashujaa wa haki na demokrasia na misingi ya utawala bora nchini,” alisema Lowassa katika taarifa yake
Mjumbe huyo wa Kamati Kuu alisema wanachama hao wa CCM walisimamia kile walichokiamini bila ya kuvunja sheria, wamekata minyororo ya unyonge na uonevu.
“Mbegu ile waliyoipanda itamea na kuzaa matunda demokrasia ya kweli nchini kwetu.
“Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba upinzani wa kweli utatokea CCM, naamini usemi huo sasa unatimia kwa kasi kubwa.
“Nawakaribisha Chadema na Ukawa kwa jumla huku kuna maisha mazuri sana, hakuna minyororo ya utumwa wa siasa. Kilichowapata ni sawa na kumpiga chura teke unamuongezea kasi tu.
“…waje wajiunge nasi katika safari ya kuleta demokrasia ya kweli na siasa zenye ukomavu, safari hii inahitaji umoja na mshikamano kufikia malengo,” alisema.
Lowassa alisema anashangazwa na namna hatua ya CCM kujinasibu kuwa CCM ikiyumba.
Alisema nchi itayumba lakini anaamini kinachotokea na jinsi CCM inavyoyumba ndivyo wananchi wanavyozidi kukomaa katika siasa na kuimarika katika harakati za kutafuta mabadiliko ya kweli.
Alisema Watanzania wa sasa hawawezi tena kuvumilia ukandamizaji wa haki zao za msingi unaofanywa na watawala.
“Nidhamu ya woga haina tena nafasi katika kujenga nchi yenye kuheshimu misingi ya haki demokasia na utawala bora,” alisema.
Juzi, CCM kilitangaza kuwafukuza wanachama wake 12, akiwamo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT), Sophia Simba, ambaye wiki iliyopita alitangaza kutogombea tena nafasi hiyo.
Wengine waliofukuzwa ni wenyeviti mikoa ambao ni Jesca Msambatavangu (Iringa), Erasto Kwilasa (Shinyanga), Ramadhan Madabiba (Dar es Salaam) na Christopher Sanya (Mara).
Waliofukuzwa wengine ni Willfred ole Mollel ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Mjini, mjumbe wa NEC wa Wilaya ya Babati Mjini, Ally Sumaye na Mathias Manga wa Wilaya ya Arumeru.
Katika orodha hiyo pia wamo wenyeviti wa wilaya wa chama hicho ambao ni Omari Awadhi (Gairo), Ally Msuya (Babati Mjini), Makolo Laizer (Longido) na Salumu Madenge (Kinondoni-Dar es Salaam).
Wanachama wengine waliochukuliwa hatua baada ya kufanya makosa kama hayo kuwa ni Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi ambaye amepewa onyo kali na anatakiwa kuomba radhi.
Wakati Nchimbi akipewa onyo, Adam Kimbisa ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma na Mbunge wa Afrika Mashariki amesamehewa.
Kutokana na uamuzi huo Sophia atalazimika kupoteza ubunge. Ilielezwa kuwa amefukuzwa baada ya kupatikana na makosa ya maadili kinyume na Katiba na kanuni za chama hicho. | 3 |
Huo ni ushindi wa pili kwa Stars katika mechi za kirafiki za kimataifa baada ya mwishoni mwa wiki iliyopita kuifunga Botswana mabao 2-0.Mabao ya Stars jana yalifungwa moja kwa kila kipindi kupitia kwa wachezaji Simon Msuva na Mbaraka Yusuf.Msuva ndiye aliyeanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 20 akiunganisha pasi ya Ibrahim Ajibu na kuachia shuti lililomzidi mlinda mlango wa Burundi, Nahimana Jonathani.Bao hilo liliiamsha Burundi ambayo nayo ikaanza kufanya mashambulizi na dakika ya 31 nusura mshambuliaji Laudit Mavugo aandike bao, lakini akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufanya hivyo shuti lake lilipaa juu na kufanya Stars kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao hilo.Mavugo aliisawazishia Burundi bao katika dakika ya 54 akitumia vema makosa ya kipa wa Stars, Deogratius Munishi ‘Dida’ aliyeacha lango ambapo Mrundi huyo alimwahi na kuujaza mpira wavuni.Bao hilo lilidumu kwa dakika 24 tu kwani Yusuf aliiongezea Stars bao la pili katika dakika ya 78 akiunganisha pasi ya Ajib na kuachia shuti ambalo liligonga mwamba na mpira kumrudia kabla ya kuuwahi na kuuweka kimiani.Ushindi huo, Stars imelipa kisasi kwa Burundi ambayo ilicheza nayo mwaka 2014 na kufungwa mechi zote.Kocha Mkuu wa Stars, Salum Mayanga aliitumia mechi hiyo kuangalia kikosi kitakachocheza mechi za kuwania kufuzu Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) zinazotarajiwa kuchezwa baadaye mwaka huu. | 4 |
MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita (pichani) amewasilisha maombi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akiomba itoe amri ya kusitisha mchakato wa kung’olewa kwenye nafasi hiyo hadi maombi yake ya msingi yatakaposikilizwa.Mwita ambaye anawakilishwa na Wakili, Hekima Mwasipu amewasilisha maombi hayo dhidi ya Mkuu wa Mkoa huo, Paul Makonda, Halmashauri ya Jiji hilo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.Wakili Mwasipo aliwasilisha maombi hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Janeth Mtega wakati maombi hayo yalipokuja kwa ajili ya kutajwa. Alidai wamewasilisha maombi hayo chini ya Hati ya Dharura na yanalenga kuwazuia Mkuu wa Mkoa na Halmashauri hiyo, kujihusisha katika mchakato wa kumng’oa kwenye nafasi ya Umeya wa jiji hilo.“Tunaomba mahakama izuie mchakato huo au hata kama kutakuwa na kikao chenye ajenda hiyo, isizungumziwe na Mkuu wa Mkoa pamoja na halmashauri wazuiliwe kufanya mchakato huo. Mahakama isipofanya hivyo mleta maombi (Mwita) hatapata haki yake ya kusikilizwa,”alidai Mwasipo.Akijibu hoja hiyo, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Gabriel Malata alidai kesi hiyo imekuja kusikilizwa chini ya Hati ya Dharura ili haki ionekane imetendeka. Alidai hawajui kama kuna kitu chochote, kinachoweza kutokea kuhusu kung’olewa kwa mleta maombi huyo. Hivyo, aliiomba mahakama kukataa maombi hayo kwa gharama.Alidai hakuna mazingira ya moja kwa moja, yanayoashiria kwamba kwenye kikao kitakachofanyika, kutakuwa na ajenda inayohusu kumtoa katika nafasi hiyo meya huyo. Hata hivyo, jopo la mawakili wa serikali tayari limewasilisha mapingamizi, kupinga maombi ya msingi yaliyopo mahakamani hapo.Hakimu Mtega aliahirisha kesi hiyo hadi leo, kwa ajili ya kutoa uamuzi, wa ama kusitisha mchakato huo au la. | 3 |
UTOAJI hati za kusafiria za kielektroniki unatarajiwa kubaini na kurejesha Watanzania wa ughaibuni wanaofanya kazi zisizo na ujuzi walioenda kwa kurubuniwa na kufanyishwa kazi kwa kudhulumiwa.Ofisa Uhusiano wa Uhamiaji, Azizi Kirondomara amesema hivi karibuni jijini Dar es Salaam kwamba, utaratibu huo wa hati za kusafiria za kielektroniki, itakuwa fursa nzuri ya kuchuja maombi kuhakikisha hakuna wanaoenda au kubaki nje ya nchi wakifanyishwa kazi kwa kudhulumiwa.“Lazima ujiridhishe anakwenda kuishi vipi,... maelekezo tuliyo nayo ni kwamba mkataba utoke alikoajiriwa na ugongwe mhuri wa ubalozi,” alisema Kirondomara wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili kwenye Maonesho ya Viwanda ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) yaliyohitimishwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam ambayo idara hiyo ilishiriki ikiwa na banda lake.Kirondomara amesema lipo kundi la mabinti na vijana wa umri wa miaka 13 hadi 25 ambao kabla kupewa hati ya kusafiria, Uhamiaji inajiridhisha kama hakudanganywa hususani malipo ya kazi watakayofanya.Alisema, wahusika katika kundi hilo pia ni lazima walete wazazi/mzazi wao waridhie.Hata hivyo alisema upo uwezekano baadhi ya wazazi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha, pia kurubuniwa.Akizungumzia utaratibu wa ubalozi kuthibitisha, alisema lazima anayeomba hati awe na mkataba wa kazi , upitishwe ubalozi, ugongwe muhuri na ubalozi wa Tanzania nchi husika na uwasiliane na mwajiri. “Sasa ukipata mkataba, unatakiwa kuupitisha ubalozini...Katika kubadilisha hati za kusafiria ndipo tutawabana. Tunajiridhisha safari za wasichana na wavulana tujiridhishe wanaenda kuishi vipi,” alisema.Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji imeimarisha udhibiti kwa kuzuia kutoka nchini vijana na wasichana wa kitanzania wanaoenda kufanya kazi zisizo za ujuzi kama vile za ndani katika baadhi ya nchi na hatimaye kujikuta wakiteswa, kunyanyaswa na kufanyishwa kazi zisizo na staha wafikapo nchi hizo.Wakati huo huo, Uhamiaji imesema inaandaa mpango wa mafunzo kwa ajili ya maofisa watendaji wa kata unaolenga kuweka udhibiti wa kutosha wa wahamiaji haramu katika maeneo mbalimbali nchini.Akizungumzia serikali za mitaa kudhibiti wahamiaji haramu, Kirondomara alisema idara inashirikiana nao na wapo maofisa uhamiaji mahususi wa ngazi ya kata wakishirikiana na maofisa wa serikali.Alisema kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM), idara imetengeneza mpango huo kuelimisha maofisa watendaji wa kata utakaoanzia Dare s Salaam kuhusu mafunzo ya uraia na uhamiaji.Alisema mpango huu wa mafunzo ukienea nchini utasaidia watendaji hao wa kata nchini kuwa na uelewa mpana juu ya kutambua wahamiaji haramu na kuelewa madhara ya watu hao kuishi nchini isivyo halali. | 3 |
Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda ameuagiza mkoa wa Pwani uanzishe ofisi itakayoziweka pamoja taasisi zote zinazowezesha uwekezaji ili kupunguza usumbufu kwa wawekezaji.Ametoa agizo hilo kwenye viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo mjini Kibaha wakati anafunga maonesho ya pili ya viwanda mkoa wa Pwani.“Huu mfumo niliouaona kwa one stop center nataka ujidhihirishe sasa kwa maana ya ofisi katika mkoa wa Pwani, watu wakija waseme nenda Pwani ukitaka kuona kinachoendelea ni nini, tukifanikiwa hilo utaona kabisa kitu hiki kimekusaidia sana” amesema Pinda.Ameeleza kufurahishwa na banda lilizoziweka pamoja taasisi hizo wakati maonesho hayo yaliyoanza Alhamisi iliyopita na amebainisha kwamba, hili lisipofanyika mwekezaji anachoka kuzunguka hata kabla ya kuwekeza.“Na nimewaomba sana, isitoshe tu kuwaoneni hapa kwenye maonyesho haya ndani ya banda moja lakini jambo hili limesisitizwa sana na Serikali zilizopita na Serikali ya Awamu ya Tano kuwa na kitu tunakiita a one stop center mwekezaji anapokuja matatizo yatatuliwe kwenye eneo moja tu kwa kuwakuta wote wahusika katika eneo hilo” amesema Pinda.Ameutaka Mkoa wa Pwani uwe mfano kwa mikoa mingine kwa kuondoa usumbufu kwa wawekezaji."Maana umeshaanza na viwanda, mwekezaj anataka kuja kuwekeza, ukifanya lile utaona wengi watapenda kuja kwenye mkoa wako kwa sababu umejenga mfumo mzuri” amesema Pinda. | 5 |
MUSWADA wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa wa Mwaka 2018, umekuwa moto katika Kamati ya Bunge, baada ya mamia ya wadau kujitokeza kutoa maoni ili kuuboresha ili ukuze demokrasia ya vyama vya siasa nchini.Akizungumza katika mahojiano jijini hapa jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mohamed Mchengelwa alisema kufurika kwa wadau wa siasa nchini ili kutoa maoni ni mwamko wa wananchi katika kukuza na kupanua demokrasia nchini.“Wadau wengi sana wa siasa nchini wamefika kutoa maoni kwenye kamati, kitendo kinachoonesha wazi kwamba wananchi wana mwamko wa kutaka maboresho ya kukuza demokrasia katika vyama vya siasa,” alisema.Alisema wao kamati wamekuwa wakiwashauri wadau kutoa suluhisho la mambo, badala ya kupeleka maswali. Pia wanawashauri wadau hao, kutoa ushauri wa kisheria na kitalaamu kuhusu vifungu wanavyoona, havijaandikwa vizuri ili viaandikwe vipi katika marekebisho ili kupata sheria hiyo ambayo italeta maendeleo ya siasa nchini.Mchengelwa ambaye ni Mbunge wa Rufiji (CCM), alisema kamati tayari imepokea maoni ya vikundi vya wadau 15 na wananchi 150 na wengi wanaendelea kujitokeza.Alisema kama hali itaendelea kama hivyo, wanaweza kufikia 300, jambo ambalo linaonesha Watanzania wameamka katika kujenga demokrasia. Mwenyekiti huyo wa Kamati alisema, kamati imefurahishwa na mwamko mkubwa katika kutoa maoni ili kuboresha muswada huo, na wao hawataacha kuyatumia maoni yao maadamu yatakuwa na malengo ya kujenga msakabali wa Taifa.Alitaja vifungu vilivyotolewa maoni sana kuwa ni pamoja na kile kinachoonesha Msajili wa Vyama vya Siasa, anapewa madaraka makubwa ya kukifuta chama. Alisema duniani kote, kuna mipaka ya kufanya siasa.Alisema kuna mambo ambayo wadau wanarudia kuyaeleza, hata kama yapo kwenye sheria ya zamani, mfano ya kusajili na kufuta chama, lakini wao wanachukua maoni yote na wanataka kutunga sheria itakayodumu kwa miaka 50 au 100 ijayo. Alisema kwa ujumla wadau wengi waliotoa maoni, wanataka itungwe sheria ambayo itawafaa, lakini hasa itaviwajibisha vyama vya siasa kwa wanachama wake ambao ni Watanzania.Akizungumzia umati uliojitokeza, Mwanasheria Mkuu wa zamani, Andrew Chenge alisema watu wengi wamejitokeza wakiwamo vijana, ambao ndio wenye taifa lao na muswada ni kwa ajili ya maslahi ya nchi yao.Chenge ambaye ni Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), alisema wadau wamejitokeza kutoa maoni, ambayo ni muhimu katika kuboresha muswada huo, kwani mustakabali wa nchi ni watu wote.Mbunge wa Mtera, Livingistone Lusinde (CCM) alisema wadau wengi wamejitokeza, lakini wengi hawakuona maoni mengine, mfano ya kusajili na kufuta vyama vya siasa vinaposhindwa kuendesha siasa, suala ambalo lipo ndani ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992.Alisema katika mfumo wa vyama vingi, msajili wa vyama vya siasa ana wajibu wa kuhakikisha vyama vya siasa vinavyoshindwa kufanya siasa au kutokuwa na wanachama wanaotakiwa pande mbili za Muungano, vinaweza kufutwa ; na hata katika sheria ya zamani, sharia hiyo ilikuwepo na baadhi ya vyama vilifutwa.Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema) alisema katika maoni yake, anaona muswada huo ungeonesha pia uwezo wa vyama kuungana, baada ya uchaguzi ili kupatikana viongozi mbalimbali wa ngazi za juu.Akizungumza wakati wa kuwasilisha muswada huo, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi alisema muswada huo umletwa, kwa lengo la kuboresha mfumo wa vyama vya siasa nchini.Alisema Jumatatu na Jumanne ijayo, watakuwa na kazi ya kukusanya maoni hayo na kuyachambua na kuona yapi yanaweza kuboresha muswada. Aliwahakikishia Watanzania kuwa hawatasita kufuta au kubadilisha kifungu, kama kitakuwa hakijawekwa vizuri katika muuswada. | 3 |
['Ajenti wa Kiungo wa Manchester United Paul Pogba anaamini "kutafikiwa suluhisho la kuridhisha hivi karibuni kwa pande zote" katika kuamua mustakabali wa mchezaji huyo. ', 'Ijumaa iliyopita, ajenti Mino Raiola taliliambia gazeti la The Times kuwa kiungo huyo mwenye miaka 26 anataka kuhama Manchester United. ', 'Pogba, ambaye yupo katika ziara ya kabla ya msimu na klabu ya Man United katika nchi za Australia, Singapore na China, alisema mwezi Juni kuwa "huu unaweza ukawa muda muafaka kuhamia kwengine". ', '"Mchezaji (Pogba) hakufanya kosa lolote," Raiola aliuambia mtandao wa Talksport. ', '"Amekuwa na heshima na weledi. Klabu imekuwa ikijua hisia zake kwa muda mrefu. ', '"Ni aibu kuwa kuna baadhi ya watu wanapenda kukosoa bila ya kuwa na taarifa sahihi, na ninasikitishwa kuwa klabu haichukui hatua yoyote kwa wanaofanya hivyo."', 'United watacheza na Perth Glory Julai 13 na kisha Leeds United Julai 17, baada ya hapo watasafiri mpaka Singapore kwa mchezo mmoja dhidi ya Inter Milan Julai 20. ', 'Watamaliza ziara yao ya maandalizi kwa mchezo mmoja dhidi ya Tottenham jijini Shanghai Julai 25.', 'Manchester United bado haijapokea ofa rasmi ya usajili kutoka klabu yeyote inayomtaka Pogba na uongozi upo kimya juu ya tetesi za usajili kumhusu mchezaji huyo mwenye thamani ya pauni milioni 89.', 'Klabu za Real Madrid na Juventus tayari zimeshatangaza nia ya kutaka kumsajili Pogba. Lakini mpaka sasa hawajatuma maombi ama kukutana na uongozi wa United kufanya mazungumzo ya usajili. ', 'Inaarifiwa kuwa Pogba amebakiza miaka miwili kwenye mkataba wake wa sasa, lakini kiuhalisia ni mitatu sababu United waliongeza uwezekano wa kusalia mpaka 2022.', 'Kipengele hicho kinawapa nguvu kubwa United kwenye meza ya majadiliano endapo Real ama Juventus watawafuata. ', 'Kwa sasa, maafisa wakuu wa United wanaonekana kuwekeza muda wao wote kwenye maandalizi ya msimu mpya na wanaamini Pogba atakuwa kwenye kikosi cha kocha Ole Gunnar Solskjaer kitakachominyana na Chlsea kwenye mchezo wa kwanza wa msimu wa 2019/2020 dhidi ya Chelsea kwenye uga wa Old Trafford Agosti 11. '] | 4 |
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imeshindwa kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, kwa sababu mshitakiwa huyo ana miadi na daktari.Akiwasilisha hoja ya kuomba ahirisho la kesi hiyo likiambatana na nyaraka za daktari mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba, Wakili wa Utetezi Peter Kibatala alidai afya ya Mbowe si nzuri na alitakiwa kuonana na daktari jana.“Mheshimiwa hali ya mshitakiwa bado si nzuri na alitakiwa kuonana na daktari lakini kwa kuheshimu amri ya Mahakama amelazimika kuomba daktari aahirishe miadi ili aweze kuhudhuria hivyo tunaomba ahirisho na kesi hii iendelee kuanzia Desemba 2 hadi 6, mwaka huu,” alidai Kibatala.Akijibu hoja hiyo, Mkurugenzi Msaidizi wa Mashitaka, Joseph Pande alidai Kibatala aliomba ahirisho Novemba 26 na kukubaliwa bila kuwepo maelezo ya miadi ya daktari hivyo inashangaza kuona taarifa hizo zikiwasilishwa jana. Alidai kama afya ya mshitakiwa ilikuwa haijakaa sawa na ana miadi na daktari ilitakiwa iwasilishwe Novemba 26, mwaka huu au wakati wowote mapema kabla ya shauri hilo.“Inashangaza taarifa hizi kuwasilishwa hapa leo nadhani taarifa hizi zilitakiwa kuwasilishwa mapema lakini kuzileta wakati huu ni kupoteza muda hivyo hatuoni sababu ya kuahirisha kesi,” alidai Pande.Mkurugenzi Msaidizi wa Mashtaka, Faraja Nchimbi alitoa hoja mbadala na kuomba mahakama iendelee na kesi hiyo kwa kufuata Kifungu cha 147 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya Tano kinachoruhusu mshitakiwa mwingine kuendelea na ushahidi.“Mheshimiwa ikikupendeza niiombe mahakama ifuate Kifungu cha 147 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya Tano kinachoruhusu mahakama imruhusu mshitakiwa aendelee na matibabu lakini iendelee kusikiliza ushahidi wa mshitakiwa mwingine,” alidai Nchimbi.Akitoa uamuzi baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, Hakimu Simba alisema kesi hiyo ni ndefu na wasipokuwa makini haitaisha hivyo aliiahirisha jana tu kinyume cha maombi ya upande wa utetezi.Kesi hiyo itasikilizwa tena leo saa nne na nusu asubuhi. Novemba 26, mwaka huu, mahakama hiyo iliahirisha kesi hiyo hadi jana kwa madai kuwa hali ya afya ya Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro, haikuwa nzuri na alihitaji kupumzika. Ilielezwa mahakamani hapo kuwa anaumwa malaria, homa ya dengue na shinikizo la damu.Mbali na Mbowe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, wabunge John Mnyika (Kibamba), John Heche (Tarime Vijijini), Halima Mdee (Kawe), Ester Bulaya (Bunda Mjini), Peter Msigwa (Iringa Mjini), Esther Matiko (Tarime Mjini) na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji.Washitakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 13 yakiwamo ya kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji jinai kati ya Februari Mosi na 16, 2018, Dar es Salaam. | 3 |
RAIS John Magufuli ametoa mwezi mmoja taasisi za serikali kuhama katika majengo ya watu binafsi isipokuwa kwa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ambayo imepewa siku tano kuhama kutekeleza agizo hilo.Ametoa agizo hilo akiwa Mji Mdogo wa Laela mkoani Rukwa jana muda mfupi kabla ya kuifungua barabara inayoiunganisha Tunduma – Laela – Sumbawanga iliyogharimu Sh bilioni 223.1.Rais Magufuli alisema ni kitu kisichowezekana ofisi hizo kuendelea kupanga katika majengo ya watu binafsi na kuyaacha majengo ya serikali yakiwa wazi, jambo aliloeleza kuwa huenda lina maslahi kwa baadhi wahusika kupeana asilimia fulani zinazotokana na kodi zinazolipwa.“Sasa hivi majengo mengi ya serikali Dar es Salaam yapo wazi lakini bado kuna baadhi ya taasisi zimeendelea kung’ang’ania kupanga katika majengo ya watu binasi, natoa mwezi mmoja muhame katika majengo hayo,” alisema Rais Magufuli.Kuhusu Tanroads, alimwagiza Mtendaji Mkuu wake, Patrick Mfugale kuhamisha ofisi zao kutoka katika Jengo la Airtel lililopo Morocco jijini Dar es Salaam na kwenda katika majengo yanayomilikiwa na serikali ili kupunguza gharama za upangaji.“Haiwezekani tangu mwaka 2000 hamna jengo. Tarura iliyoanzishwa hivi karibuni imeanza mchakato wa kuwa na majengo yake…nakupa siku tano muhame hapo mlipo na muende katika majengo ya serikali,” Rais Magufuli alimuagiza Mfugale ambaye alikuwapo jana katika shughuli hiyo ya Laela.Uchunguzi wa gazeti hili umebaini uwepo wa majengo mbalimbali hususani katika Jiji la Dar es Salaam ambayo yapo wazi baada ya wizara kuhamia Makao Makuu ya Ncihi jijini Dodoma na hivyo kuyafanya majengo hayo kubaki pasipo matumizi yoyote. | 3 |
Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam Kesi ya matumizi mabaya ya inayomkabili Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando inatarajia kuanza kusikilizwa mfululizo Aprili 24 na 25, mwaka huu. Kesi hiyo iliyokuwa inasikilizwa mbele ya Hakimu Mfawidhi, Victoria Nongwa imehamishiwa kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo leo Jumatano Machi 28, ilikuja kwa ajili ya kuanza kusikilizwa. Akiiwakilisha Jamhuri, Wakili wa Serikali kutoka Takukuru, Leonard Swai aliomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuleta mashahidi. Hakimu Shaidi amesema mahakama itasikiliza kesi hiyo mfululizo siku mbili kuanzia Aprili 24 na 25 mwaka huu hivyo Jamhuri wanatakiwa kuita mashahidi wa kutosha siku hizo. Tido anakabiliwa na mashtaka matano yakiwa matumizi mabaya ya madaraka ambapo Juni 16, 2008 akiwa Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Tido ambaye alikuwa Mkurugenzi wa TBC, kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila ya kupitisha zabuni, kitu ambacho ni kinyume na Sheria ya Manunuzi na kuinufaisha BVl. | 3 |
WATANI wa jadi Simba na Yanga, kila mmoja anatafuta namna ya ‘kuchomoka’ kwenye mechi yao ya Ligi Kuu mwishoni mwa wiki hii kwa kila mmoja akipanga mbinu zake.Miamba hiyo inatarajiwa kumenyana Jumapili ya wiki hii kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam katika mechi yao ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu. Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems aliyeamua kupiga kambi yake jijini Dar es Salaam, ameamua kukiongezea kikosi chake dozi ya mazoezi na sasa badala ya kufanya mara mbili kwa siku, itakuwa mara tatu kuanzia jana, leo na kesho ili kuivuruga Yanga katika mchezo huo.Akizungumza kwenye mazoezi ya timu yake yanayofanyika uwanja wa Boko Veterani, Aussems alisema mchezo huo ni muhimu kwa mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo lakini kwake anauchukulia kawaida na kujiandaa kama ilivyo kwa mechi nyingine.“Kila mmoja yuko imara, tunafanya mazoezi katika hali ya hewa nzuri, tunajiandaa vyema dhidi ya Yanga na ni mchezo ambao ni muhimu kwetu kushinda haina tofauti na mingine, tunachohitaji kwetu ni pointi tatu,” alisema. Alisema wanajiandaa kufanya vizuri na anaamini baada ya dakika 90 mshindi atajulikana.Kocha huyo aliongeza kuwa ameridhishwa na kambi yao ya mazoezi iliyoko Kunduchi kwani kuna hali ya hewa nzuri inayovutia na mazingira ni tulivu kwao. “Kuna utofauti gani wa kwenda kwingine kubadilisha mazingira na kukaa hapa kwenye mazingira tulivu na hali ya hewa nzuri, tunaendelea vizuri na tunafurahia maandalizi yetu,” alisema.Kwa upande wa kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera alisema hana hofu na Simba kwani ameifahamu kupitia mikanda ya video. Yanga imeweka kambi yake Morogoro na inatarajiwa kurejea kesho kwa ajili ya mechi hiyo. “Nimekuwa nikiisoma Simba kupitia mikanda ya video niliyoomba nipatiwe kila baada ya mechi yao, kwa hiyo sina hofu naamini maandalizi tunayoyafanya yatatusaidia kuibuka na ushindi,” alisema.Timu hizo zinakutana kwa mara ya kwanza zikiwa na makocha wapya kila mmoja akiingia uwanjani akiwa na historia yake tofauti katika mechi zilizopita. Aussems ameiongoza Simba kushinda michezo mitatu kati ya mitano, akipata sare moja na kupoteza mmoja dhidi ya Mbao huku Zahera anaiongoza Yanga ikitoka kushinda mechi zote nne ilizocheza. Mara ya mwisho timu hizo zilikutana Aprili mwaka huu ambapo Simba ilishinda bao 1-0 lililofungwa na beki Erasto Nyoni. | 4 |
SERIKALI itaokoa kiasi cha Sh bilioni 400 mpaka Sh bilioni 675 kwa mwaka za mahitaji ya mafuta ya kula nchini yanayoagizwa kutoka nje ya nchi baada ya kuwepo kwa mkakati wa kuongeza uzalishaji wa mazao ya alizeti na michikichi nchini.Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Ilonga (Tari Ilonga), kilichopo Kilosa mkoani Morogoro, Dk Joel Meliyo amesema hayo alipokuwa akizungumza katika Siku ya Maonesho ya Kilimo Biashara yaliyofanyika katika kituo hicho hivi karibuni.Dk Meliyo amesema mojawapo ya majukumu ya kitaifa ya kituo hicho ni uzalishaji wa mbegu bora ya mazao ya mafuta, hususani alizeti ambayo kwa kuanzia kituo hicho kimepanda ekari 83 za alizeti kati ya hizo ekari 20 kwa ajili ya mbegu za awali na ekari 63 kwa ajili ya mbegu iliyothibitishwa ubora.Alisema kwa sasa nchi inatumia tani 485,000 za mafuta ya kula kwa mwaka, hivyo kwa miaka mitano kuanzia sasa wanakusudia kupunguza uagizaji wa mafuta nje ya nchi angalau kwa nusu ya mahitaji yaliyopo.“Tunataka kuzalisha mbegu. Tunataka kuhakikisha tani zote zinazotakiwa kwa ajili ya alizeti zinapatikana. Hivyo tunatakiwa kupanda ekari laki nane ndio kutakuwa na utoshelevu wa mafuta,” alisema.Mratibu wa Utafiti wa Alizeti nchini wa Tari Ilonga, Mulamila Reuben amesema kwa sasa mahitaji ya mafuta ya kula nchini yanaongezeka mwaka hadi mwaka kadri idadi ya watu inavyoongezeka.Alisema mkakati uliowekwa na serikali ni kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula nchini kupitia kilimo cha zao la alizeti na michikichi.“TARI kupitia vituo vyake vya TARI Ilonga na TARI Kihinga vimepewa jukumu la kuratibu utafiti wa alizeti (TARI Ilonga) na utafiti wa michikichi (TARI Kihinga),” alisema.Alisisitiza kuwa kwa kiasi cha mafuta kinachozalishwa nchini zao la alizeti huchangia asilimia 70 na mazao mengine huchangia asilimia 30.“Mazao hayo ni pamoja na zao la Mchikichi, pamba, ufuta na karanga. Hivyo ni muhimu sana kuwekeza kwenye zao la alizeti ambalo linaweza kulimwa na kuzalishwa kila mwaka kwa muda mfupi na maeneo mengine huzalishwa mara mbili kwa mwaka,” alisema. | 5 |
Simba ambayo inashika nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa na pointi 62 sawa na Yanga inayoongoza kwa uwiano mzuri wa mabao, inapewa nafasi kubwa ya kushinda, kutokana na malengo ya kutaka kuwavua ubingwa Yanga ingawa kwa idadi ya mechi walizobakiwa nazo ukilinganisha na Yanga wanahitaji miujiza. Hiyo ni mechi ya 29 kwa Simba endapo watashinda watafikisha pointi 65 na kurudi kileleni kwa muda kwani kesho Yanga itacheza na Mbeya City na ikishinda itarudi tena kileleni kwa uwiano mzuri wa mabao.Matumaini ya Simba kuendelea kuwepo kwenye mbio za kuwania ubingwa ni kushinda mechi ya leo, lakini ikiomba Yanga kesho ivurunde licha ya kwamba jambo hilo ni gumu. Kocha wa Simba Joseph Omog, amesema mchezo wa leo wameupa umuhimu hivyo pamoja na kuwa na nafasi ndogo ya ubingwa lakini watapambana ili kuhakikisha wanashinda mechi zao mbili zilizosalia. “Nitatumia kikosi kamili kwasababu ligi bado inaendelea na japo nafasi ni ndogo ya ubingwa lakini hizi ni mbio lazima tupambane hadi dakika ya mwisho kwani mpinzani wetu anaweza kupoteza ikawa faida kwetu,” alisema Omog.Pia Omog alisema kikosi chake hakitakuwa na mabadiliko makubwa na kile kilichocheza mchezo uliopita dhidi ya African Lyon, ambao walishinda kwa mabao 2-1. Kocha wa Stand United Athuman Bilal ametamba kuyeyusha ndoto za Simba kuwania ubingwa. Bilali alisema hawawezi kukubali kupoteza mchezo huo kwani hata wao wapo katika hali mbaya na wanahitaji pointi tatu ili kujiweka salama na janga la kushuka daraja msimu huu.“Ni mchezo mzuri na mgumu timu yangu imejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo na utakuwa na ushindani lakini tunahitaji pointi tatu au ikishindikana basi tupate hata moja naamini itatusaidia kuondoka katika janga la kushuka daraja,” alisema Bilali. Pia Bilali alisema amekuja na nyota wake wote akiwemo Adam Kingwande, Amri Kiemba na Jacob Masawe hivyo anatarajia kutoa presha kubwa kwa wapinzani wao Simba ambao wataingia kwa nguvu ya kutaka mabao ya mapema.Mchezo mwingine leo utakuwa kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi ambapo wenyeji Azam FC wataialika Toto Africans ya Mwanza. Mchezo huo ni muhimu kwa Toto ambayo ipo kwenye ukanda wa kushuka daraja ikiwa na pointi 29 kwenye msimamo wa ligi katika nafasi ya 15. Fainali na Juventus ni maalumu - Zidane | 4 |
WIZARA sita zitashirikiana kufanya sensa ya kilimo na mifugo Novemba, mwaka huu, Tanzania Bara na Visiwani. Akizungumza katika semina ya siku mbili ya wahariri na waandishi kutoka mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma, jijini hapa jana, Mtakwimu Mwandamizi kutoka Idara ya Takwimu za Kilimo, Samweli Kawa alisema hiyo ni muhimu kupima kiwango cha umasikini nchini. Pamoja na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, wizara nyingine zitakazoshiriki katika sensa hiyo ya kilimo na mifugo ni Wizara ya Kilimo, Viwanda na Biashara, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar (OCGS). Alisema sensa hiyo itahusisha mazao yote makubwa ya kilimo yakiwemo ya chakula, biashara na mazao ya bustani, mifugo aina zote, wafugaji wa samaki, nyuki na shughuli za jamii nchini. Alisema wakulima wadogo waliochaguliwa ni wenye mashamba ya mita za mraba 25 na mifugo kuanzia ng’ombe mmoja, mbuzi 50 na kuku 100 na kingine katika kaya na familia hizo. Kawa alisema sensa hiyo ni ya sampuli, itahusisha wakulima wakubwa na wadogo, wakulima wakubwa mashamba yatapitiwa na madogo yatachukuliwa machache kwa niaba ya mengine.Alisema takwimu za sensa hiyo pamoja na kutumika katika mipango ya serikali, zitatumika vyuoni kutoa mafunzo, uzalishaji na ufugaji; ufugaji wa samaki na nyuki na wadau. Alisema sensa hiyo itakuwa ya tano tangu kuanza, nyingine zilifanyika mwaka 1971/1972, 1993/1994, 2003/2004, 2007/2008 na hii ya mwaka huu 2018/2019 itakuwa ya tano.Alisema maandalizi yamefanyika kwa kuorodhesha kaya zitakazohusika, Tanzania Bara na Zanzibar, sampuli za kaya, na majaribio tayari ya madodoso yameshafanyika katika mikoa sita Bara na miwili Kaskazini Unguja na Kusini Pemba Visiwani. Alivitaka vyombo vya habari kuwa mabalozi kwa kuelimisha umma kushiriki na kutoa ripoti ya taarifa mbalimbali kuhusu sensa hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa. Mtakwimu Mkuu wa NBS, Dk Albina Chuwa alisema mafunzo hayo ya wahariri na waandishi yanalenga kuwajengea uwezo wa kuandika kwa usahihi takwimu zinazotolewa na ofisi hiyo.Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Daniel Andrew alisema mabadiliko ya sheria NBS tangu ile ya mwaka 1995 hadi ya 2019 yanalenga kupanua wigo wa upatikanaji wa takwimu hizo.Mwanasheria kiongozi wa NBS, Oscar Mangula alisema mabadiliko ya sheria mwaka 2019, yameruhusu taasisi kutolazimika kuripoti NBS wakati zinaenda kufanya utafiti nchini. | 3 |
SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT) limetangaza majina ya wachezaji 28 watakaounda timu ya taifa kwa ajili ya maandalizi ya kushiriki mashindano ya Dunia ya Mbio za Nyika yatakayofanyika Denmark, Machi 30 mwaka huu.Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday amesema mjini Moshi kuwa timu hiyo itakuwa chini ya jopo la makocha saba, na imechaguliwa baada ya mashindano ya wazi ya taifa ya mbio za nyika yaliyofanyika juzi chini ya udhamini wa DStv pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.Gidabuday alisema kuwa timu hiyo inajumuisha idadi hiyo ya wachezaji ambao wako katika Makundi manne ya umri na umbali tofauti tofauti, ambali wako wavulana na wasichana wenye uri chini ya miaka 18 na ile ya wakubwa wa jinsi zote huku pia kutakuwa na timu ya kupokezana vijiti, ambayo itaundwa na wachezaji kutoka makundi hao.Wanariadha watakaounda kundi la wanaume weneye umri wa zaidi ya miaka 18 ni Faraja Damas, Joseph Panga, Sylvester Marco na Stephano Huche (Arusha), Deogratius Nade (Manyara), Yohane Elisante (Arusha) na Bazil Sule (Polisi).Kwa upande wa wanawake katika kundi hilo la wakubwa waliopo ni Failuna Abdi (Arusha), Magdalena Shauri (JKT), Anjelina Daniel, Amina Mohamed, Marselina Issa na Neema Msuad (Arusha).Kundi la wavulana chini ya miaka 18 litakuwa na wachezaji saba, ambao ni Michael Kishimba (Arusha), Daniel Sinda (Arusha) Emmanuel Joseph (Manyara) Francis Damiano (Mbulu), Saimon Francis (Arusha) na Nicodemo Joseph (Mbulu) wakati wasichana watakuwa ni Agnes Protus (Arusha), Anastazia Ndoromongo (Arusha), Aisha Luguna (Arusha), Sara Hiti (JKT), Gace Jackson (JKT), Noela Lemmy (Arusha) na Catherine Philipo (Manyara).Kambi hiyo itakuwa chini ya jopo la wataalamu wanane wakiongozwa na Kocha Mkuu Meta Petro kutoka Klabu ya Riadha ya Rift Valley.Wengine ni Anthony Mwingereza (JWTZ), Andrea Panga (JKT), Thomas Tlanka (Arusha) na Juma Jambau (Singida).Mwanariadha wa zamani Marcelina Gwandu ameteuliwa kuwa matroni wa kambi hiyo, huku Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Hamad Ndee akipewa jukumu la kuratibu mafunzo hayo.Kambi hiyo inatarajia kuanza Februari 20 Arusha na wachezaji wote waliotajwa katika timu hiyo wanatakiwa kuripoti katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kwa ajili ya maelekezo kabya ya kuanza rasmi kwa kambi hiyo.Akizungumza baada ya mashindano hayo, Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania (DStv), Johnson Mshana amesema DStv imekuwa ikishiriki kwa muda mrefu sasa katika kuinua mchezo wa riadha hapa nchini na kwamba ushiriki wao katika kufanikisha mashindano hayo ni katika mkakati wake endelevu wa kuhakikisha kuwa vipaji vya wanariadha wetu vinakuzwa na hatimaye kuweza kuliletea taifa medali katika mashindano ya kimataifa.“Tuna mkakati kabambe wa ‘Ni Zamu Yetu’ ambao lengo lake kubwa ni kuhakikisha kuwa wimbo wetu wa taifa unapigwa katika Michezo ya Olimpiki, hii ikiwa na maana kuwa nchi yetu inapata media tena ya dhahabu ili kupigiwa wimbo wa taifa katika michezo hiyo,” amesema Mshana.Kambi ya timu hiyo mjini Arusha inafadhiliwa na DStv pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. | 4 |
Na MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umesema upo tayari kumsaidia kisheria aliyekuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Madeke, Hosea Manga (10), mkazi wa Kijiji cha Madeke Kata ya Mfriga wilayani Njombe, anayedaiwa kupigwa na kuning’inizwa kichwa chini miguu juu na mwalimu anayetajwa kwa jina la Focus Mbilinyi, miaka miwili iliyopita na kusababishiwa kuvunjika uti wa mgongo. Tukio hilo ambalo limedaiwa kufanywa na mwalimu huyo ambaye kwa sasa inasemekana amehamishiwa Kata ya Mtwango, lilitokea Machi 21, mwaka 2017 wakati Hosea akiwa na umri wa miaka (8) ambapo mtuhumiwa huyo anadaiwa kumwadhibu viboko kumi baada ya kukosa hesabu. Akizungumza na gazeti hili Mratibu wa THRDC ,Onesmo Olengurumwa, alisema mtandao huo huwa una utaratibu wa kuwasaidia watu wanaohitaji msaada wa kisheria kwa kufuata taratibu ambazo zimewekwa. “Sisi tukipata taarifa kuhusu kesi kama hiyo tunatumia wanachama wetu ambao ni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ambapo tutawatumia taarifa za namna ya tukio lilivyotokea ambazo tunakuwa tumezipata kutoka kwa wahusika na wao najua watakapoanzia na kwa tukio hili kuna watu maalumu ambao wanawasaidia watoto,” alisema Olengurumwa. Alisema ili wahusika waweze kushughulikiwa tatizo lao wanapaswa kuwa na nyaraka zote za muhimu na taarifa kamili ya tukio zima ikiwezekana wanaweza wakatoa mawazo yao nini wanahitaji. Kauli ya THRDC imekuja wakati ambao baba mzazi wa mtoto huyo, Hosea Manga, akidai kuwa pamoja na kuendelea kumtibia mtoto wake lakini anahitaji msaada zaidi ili haki itendeke kwa kuwa kesi ya Jinai namba 83 ya mwaka 2017 waliyoifungua ili kumshtaki mwalimu huyo katika Mahakama ya Mkoa wa Njombe ilifutwa. Alisema kesi hiyo ilifutwa baada ya daktari aliyemtibu mtoto huyo mara ya mwisho katika Hospitali ya Muhimbili kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi licha ya kuitwa mara nane. Gazeti hili pia bado linaendelea kumtafuta Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Ole Sendeka, ambaye aliahidi kulishughulikia suala hilo kwa kuwa alishapokea malalamiko hayo ofisini kwake. Mbali na Ole Sendeka, Mwanasheria Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Wakili Helman Danda, alikiri kesi hiyo kufutwa kwa sababu Jamhuri ilishindwa kupeleka shahidi ambaye ni daktari wa mwisho aliyemtibia mtoto huyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam. “Ni kweli nimefuatilia nimeona kesi ilifutwa na sababu ni upande wa ushahidi ambaye ni daktari wa Muhimbili kushindwa kuja kutoa ushahidi, kwa mazungumzo zaidi mtafute Mkuu wa Mkoa,” alikaririwa Mwanasheria huyo alipozungumza na mwandishi wa gazeti hili mkoani Njombe. Mwandishi wa gazeti hili alifika nyumbani kwa mtoto huyo aliyekuwa akisoma darasa la tatu Kijiji cha Madeke umbali wa kilomita 103 kutoka Njombe mjini mapema. Akizungumza na gazeti hili mtoto huyo alisema tukio hilo lilitokea Machi 21 mwaka 2017 akiwa na umri wa miaka (8) ambapo alipigwa na mwalimu kwa sababu ya kukosa hesabu. Alisema siku ya tukio akiwa darasani kwenye kipindi cha somo la hesabu lililokuwa likifundishwa na mwalimu aliyemtaja kwa jina la Focus Mbilinyi ambaye aliwataka kufanya majaribio, yeye na wenzake wawili walikosa hesabu zote 10. “Ilikuwa asubuhi tukiwa darasani tunasoma somo la hesabu mwalimu alitupa hesabu 10 na akasema ukikosa utachapwa kulingana na hesabu ulizokosa, hivyo mimi nilikosa hesabu zote na kutakiwa kuchapwa fimbo 10, mwalimu wakati anatuchapa, tulikuwa watatu, alituning’iniza kichwa chini miguu juu katika moja ya dirisha la darasani ndipo nilipoangukia mgongo na kuhisi maumivu makali yaliyosababisha hadi leo natumia muda mwingi nikiwa hapa kitandani,” alisema Hosea. Kwa sasa mtoto Hosea anatumia muda wake mwingi akiwa amelala kitandani kutokana na maumivu makali anayoyapata baada ya tukio hilo la kuumia mgongo lililosababisha kutokea kwa kidonda kikubwa sehemu ya chini unapoishia uti wa mgongo. Zaidi wakati wote wa ugonjwa wa takribani miaka miwili, ameshindwa kuendelea na shule. | 0 |
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40) na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu. | 5 |
Na KULWA MZEE DAR ES SAALAM MAHAKAMA Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu uchumi, maarufu ‘Mahakama ya Mafisadi’ imemtia hatiani na kumuhukumu raia wa Nigeria, Christian Ugbechi (28) kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kusafirisha pipi 56 za dawa za kulevya aina ya heroin hydrochloride. Hukumu hiyo ilitolewa jana mbele ya Jaji Sirrilius Matupa baada ya Mahakama kuridhishwa kwamba upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha kosa pasipo kuacha shaka. Alisema ili kuthibitisha makosa hayo upande wa mashtaka uliita mashahidi wake 11 waliofika mahakamani na vielelezo 22. Mahakama hiyo imeamuru dawa za kulevya alizokutwa nazo mshtakiwa ziteketezwe kwa mujibu wa sheria. Akisoma hukumu hiyo, Jaji Matupa alisema mahakama imemuhukumu mshtakiwa kutumikia kifungo cha miaka 30 gerezani na si kifungo cha maisha kwa sababu imeona inayo mamlaka ya kumpa mshtakiwa adhabu kwa jinsi yenyewe inavyoona kutokana na mkanganyiko uliopo kwenye kifungu cha sheria cha 15(1)(a) na 15(1). “Sheria hizo mbili zilikuwa na madhumuni tofauti kutokana na matumizi ya maneno hayo shall be liable ambayo yako kwenye kifungu cha 25(1)(a) na shall be sentenced kifungu cha 15(1),”alisema. Mshtakiwa Ogbechi alitiwa hatiani, Juni 19 na jana amesomewa adhabu yake ambapo upande wa mashtaka uliwakilishwa na Wakili wa Serikali, Batilida Mushi huku utetezi ukiwakilishwa na Wakili Nashon Nkungu. Wakili wa utetezi, Jeremiah Mtobesya aliiomba mahakama kumpunguzia adhabu mshtakiwa licha ya kwamba kifungu cha sheria cha 15(1) kinaamuru mshtakiwa kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani lakini siyo lazima, itolewe adhabu hiyo, mahakama inaweza kuamua vinginevyo kutokana na maneno yaliyopo kwenye kifungu cha 15(1)(a). Mahakama ilisema pamoja na mshtakiwa kujitetea kwamba alifanyiwa upekuzi mara tatu na hakukutwa na kitu chochote na hivyo upande wa mashtaka ulipaswa kuleta ushahidi wa CCTV, haikuwa lazima kuwapangia upande wa mashitaka mashahidi wa kuwaleta na kwamba walikuwepo mashahidi wengine waliothibitisha mashitaka. | 2 |
Na GABRIEL MUSHI “SIWEZI kufanya kazi ya kusomesha wazazi. Hata kama ni mtoto wangu, siwezi kumfundisha. Hilo haliwezi kutokea ndani ya utawala wangu. Sikumpeleka mtoto shule ili apate mimba. Ninatoa elimu ya bure kwa wanafunzi ambao wameamua kusoma.” Hiyo ni kauli aliyoitoa Rais John Magufuli Julai mwaka huu mkoani Pwani. Licha ya kauli hiyo kuzua mjadala kutoka kwa wadau mbalimbali wa elimu na afya nchini, inabainisha mojawapo ya madhara ya ndoa na mimba za utotoni kuwa ni kukosa haki ya kuendelea kupata elimu kwa wakati sahihi. Mimba na ndoa za utotoni ni wakati msichana anapopata mimba au kuolewa kabla ya umri wa miaka 18. Mara nyingi kuna matokeo mabaya ya kimwili na kiakili kwa mama na mtoto wakati wa ujauzito, ambayo yanaweza kuepukwa kama msichana atusubiri mpaka atakapofikia umri sahihi. Tatizo la ndoa na mimba za utotoni limekuwa likiongezeka kila mwaka na kutajwa kusababisha umaskini mkubwa katika familia na mataifa mengi katika Bara la Afrika. Tatizo hili hili pia limekuwa likichangia vifo vya mabinti wengi katika jamii zetu. Kwa mujibu wa Shirika la Idadi ya Watu katika Umoja wa Mataifa (UNFPA), kila mwaka watoto milioni 7.3 wa kike chini ya miaka 18 hushika mimba. Huku katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Tanzania na Uganda ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa changamoto za mimba za utotoni. Pia takwimu za utafiti wa demografia ya afya (TDHS) wa mwaka jana, zinaonesha kuwa asilimia 36 ya wasichana wenye umri kati ya miaka 20-24 waliolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18. Tatizo limekuwa kubwa vijijini japokuwa hata mijini lipo kwa kiwango kidogo. Takwimu zinaonesha kuwa kasi ya ufungaji wa ndoa hizo kwa Mkoa wa Shinyanga ni asilimia 59, Tabora asilimia 58, Mara asilimia 55, Dar es Salaaam asilimia 17 na Iringa asilimia nane. Tatizo ni nini? Mratibu wa masuala ya uelimishaji wasichana kutoka Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Amina Ally anasema moja ya visababishi vya mimba na ndoa za utotoni ni kiwango kidogo cha elimu ya afya ya uzazi. Anasema wazazi wamekuwa waoga kuzungumza moja kwa moja na watoto wao kuhusiana na masuala ya uzazi, hivyo mtoto anapoanza kupata mabadiliko ya mwili wazazi hawana nafasi kuongea nao. “Pia baadhi ya mambo yanayochangia mimba na ndoa za utotoni ni umaskini, tamaa, kufanya ngono zembe, shinikizo rika na utamaduni. “Kutokana na hali hiyo, CDF tumeanzisha mradi wa kuelimisha jamii katika Kata ya Kitunda iliyopo jijini Dar es Salaam ili kuhakikisha kukomesha vitendo hivi. “Mradi huu uliofadhiliwa na ubalozi wa Uholanzi unatekelezwa katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa sababu unakabiliwa na tatizo hili kwa asilimia 19 na Kitunda ni eneo ambalo wakazi wengi ni watu wenye tamaduni na desturi za mikoa ya kanda ya ziwa inayoongoza kwa kuwaozesha watoto wao mapema,” anasema. Wasichana wafunguka Wakizungumza na MTANZANIA baadhi ya wasichana wanaoishi katika kata hiyo, wanasema mbali ya utandawazi pia tamaa ya kuolewa imekuwa mojawapo ya chanzo cha mimba za utotoni. Mmoja wa wasichana hao, Adela Anthony (17), anasema mabadiliko ya teknolojia, mfumo wa maisha na mila zimewaathiri. “Mtoto wa miaka 16 anaolewa. Kama mzazi anamuoza, mtoto huyo atapata mimba wakati sheria zetu zinasema msichana mwenye umri chini ya miaka 18 bado ni mtoto. Naye Josephina Damian (19) ambaye amemaliza kidato cha nne mwaka jana anasema mimba za utotoni zimesababisha marafiki zake watatu kushindwa kuhitimu elimu ya sekondari. “Marafiki zangu watatu tulikuwa tunasoma wote waliishia kidato cha tatu baada ya kupata mimba, hali hii inatokana tamaa ya fedha na wazazi kutowapatia elimu ya uzazi ili wajitambue miili yao. Aidha, Julieth Paulo anasema baadhi ya wasichana huingia kwenye uhusiano kwa tamaa ya kutaka kuolewa ili hali hawajatimiza umri sahihi. “Tunaona utandawazi umeathiri, mabadiliko ya teknolojia tunayatumia vibaya, mtoto wa miaka 10 anamiliki simu ya kijanja (smart phone) anangaalia picha na video za ngono na mambo mengine, vile vitu anavyoviona anaanza kwenda kuvifanya kwa vitendo, laiti wazazi wangekuwa na uwezo wa kuelimisha watoto wao wasingewapa nafasi ya kutumia simu hizo,” anasema. Madhara ya tatizo Amina kutoka CDF anafafanua kuwa yapo madhara yanayoweza kumpata msichama pindi anapopata mimba chini ya umri wa miaka 18. Anasema wasichana wanaoolewa au kupata mimba za utotoni hupoteza fursa na haki ya elimu. Wengi wao hufukuzwa shuleni au wazazi wao kupoteza imani kwao kiasi kwamba husita kuwaendeleza kimaisha hata baada ya kujifungua, hali hii hufungua mlango kwa msichana kuingia katika umaskini na kuzaa ovyo bila mpangilio. “Pia hupata madhara kimwili kwa kuwa hawajawa tayari kuyakabili majukumu ya uzazi na unyumba kwa sababu nyonga za wasichana wanaoendelea kukua mara nyingi huwa changa na finyu kiasi kwamba husababisha matatizo mengi ya uzazi wakati wa kujifungua kwa njia ya kawaida. “Wasichana wengi huchelewa kujifungua au uchungu huchukuwa saa nyingi kabla ya kujifungua, hali hii inaweza kusababisha kifo cha mama au mtoto au wote wawili kama matibabu ya dharura ya upasuaji kwa ajili ya uzazi hayakufanyika. Idadi kubwa ya akina mama wanaojifungua kwa njia ya upasuji ni wale walio na umri mdogo.
“Wasichana wanaopata ujauzito na kujifungua katika umri mdogo wengi wao pia hupata tatizo la fisitula, ambayo husababisha msichana kutokwa na haja ndogo au kubwa bila kujizuia. Uambukizo wa bakteria katika njia ya kizazi pamoja na kupata kifafa cha mimba. Huzaa watoto wenye uzito pungufu au njiti. Pia wasichana wanaozaa katika umri mdogo hupata hali ya aibu na hisia ya kudharauliwa. Jitihada za Serikali Kumekuwapo na jitihada mbalimbali za kuokoa watoto wa kike kutumbukia katika mimba na ndoa za utotoni. Hatua ambazo zimechukuliwa, kutunga sheria ya mitandao, inayozuia watu kutumiana picha za ngono, pia nchi za Afrika Mashariki baadhi zimeridhia hatua hizo lengo ni kujaribu kutengeneza maadili ya watoto. Naye Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu anasema: “Tunataka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, lakini hatutaweza kuwa na nchi yenye viwanda wakati watoto 36 katika kila watoto 100 nchini wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18 na watoto 27 wa Kitanzania wanapata mimba kabla ya umri huo, hili ni tatizo kubwa ambalo athari zake zitaonekana baadae.” Akizindua ripoti ya utafiti kuhusu athari za mimba na ndoa za utotoni ambao ulifanywa kwa ushirikiano kati ya CDF na wizara yake katika kuhakikisha ndoa hizo zinakoma, ameanza kutumia marekebisho ya Sheria ya Elimu yaliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Juni mwaka jana, ambayo yanakataza mtu yeyote kumuoa mwanafunzi wa elimu ya msingi au sekondari kwa kuwa ni kosa la jinai lenye adhabu ya miaka 30 jela. | 0 |
ZAIDI ya mabasi 2,840 yanayokwenda mikoa mbalimbali nchini yamefungwa mfumo maalumu wa ufuatiliaji wa mwenendo wake (VTS) na umeanza kutumika rasmi jana.Mfumo huo ulioanza Januari mwaka juzi kwa majaribio kwa baadhi ya njia, ni maalumu kubaini madereva wanaoendesha zaidi ya kasi ya mwendo wa 80 kwa saa ili kuepusha ajali zinazotokana na mwendokasi. Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na nchi kavu (Sumatra), Gilliard Ngewe alisema wakati majaribio yalihusisha mabasi yanayotoka Dar es Salaam kwenda mikoa ya Kanda ya Ziwa, hivi sasa mabasi 2,840 yote nchini yameunganishwa. Ngewe alisema utafiti mbalimbali uliofanyika, umebainisha upo umuhimu kutafuta njia za kudhibiti ajali hizo.Alisema miongoni mwa utafiti ni pamoja na uliofanywa na Sumatra kwa kupitia taasisi ya BICO ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unaoonesha asilimia 76.4 za ajali hizo zilitokana na makosa ya kibinadamu. Kwa mujibu wa meneja wa mradi huo, Godfrey Nsato mfumo huo wa VTS ni muhimu kudhibiti madereva nchini na kupunguza ajali za barabani.Alisema mfumo huo utatoa hadhari iwapo dereva atatanua njia kwa lengo la kuwahi na akiwa kwenye mwendo wa kasi itampigia ishara ya kumjulisha kuwa amezidisha mwendo, itaonesha pia iwapo dereva alikuwa akienda hovyo barabarani, kutoa taarifa ya ajali na itamtambua dereva wa basi. Alitaja faida nyingine za mfumo huo kuwa umesaidia kupunguza matukio ya ajali, kupunguza athari za ajali na kupunguza matumizi ya mafuta kwenye mabasi. Hata hivyo Nsato alisema baadhi ya madereva wamekuwa wakihujumu mfumo huo na kusababisha athari za ufanisi.Alisema pia kuna uhitaji wa maboresho ya elimu, udhibiti na usimamizi wa sheria kwa madereva na watumiaji wengine wa barabarani. Hii ni kutokana na utafiti huo kubaini kuwa baadhi ya madereva hawapatiwi mafunzo ya kutosha. Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Dk Isack Kamwele ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, alisema wadau wote nchini waungane kuhakikisha wanamaliza tatizo la ajali barabarani.Kamwele ameagiza kila mmiliki wa basi kuwa mwaminifu na kufunga mabasi yake mfumo huo na iwapo itabainika kuwa kuna waliokiuka, Sumatra iwachukulie hatua kali kwa mujibu wa sheria. Kamwele ameshauri pia magari yote ya serikali na daladala kufungwa VTS na kwamba serikali inaunga mkono juhudi za kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua zaidi kama sio kumalizika. | 3 |
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM BENKI ya I&M Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, lakini inang’ara kwa kutoa bidhaa na huduma za kipekee ambazo zinakidhi mahitaji yote ya mteja katika soko. I&M Tanzania ilitambulisha akaunti mpya ya wanawake ya Tunaweza inayotoa suluhisho kwa wanawake wa ngazi zote kuanzia mmoja mmoja, wajasiriamali hadi kikundi au taasisi. Akaunti hiyo inajitofautisha kwa kutoa huduma bila malipo yoyote, haina makato ya kila mwezi na viwango vyake vya riba vinavutia kwenye akiba. Akizungumza leo jijini Dar es Salaa, katika maonyesho hayo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo, alisema kuwa bidhaa hiyo mpya imeunganishwa kwenye mtandao wa benki wa kidijitali ili kuwapa wateja huduma bora na endelevu wakati wowote wanapohitaji. Alisema I&M Tanzania ni sehemu ya I&M Holdings Kenya iliyoanzishwa mwaka 1974 kama kampuni ya huduma za kifedha kabla baadaye kubadilishwa kuwa benki ya biashara. “Mwaka huu inasherehekea miaka kumi ya huduma zetu katika soko la Tanzania. Tunafurahi kuendelea kuhudumia wateja wetu na wateja wapya, pia tunashukuru wateja wetu na washikadau wote walioshiriki katikakuiletea benki mafanikio makubwa kwa kipindi chote cha miaka kumi kwenye soko.” “Tunatoa huduma kadhaa za kifedha ikiwa ni pamoja na akaunti ya akiba, current akaunti kwa madhumuni ya biashara, mikopo ya biashara, huduma za kubadili fedha, uhamishaji fedha kitaifa na kimataifa, huduma za kidijitali ambazo hutoa fursa kwa mteja kupata huduma za benki kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *150*32# au kupitia iClick- huduma ya benki kwa njia ya mtandao inayopatikana bila kikomo kwa saa 24,” alisema Anitha Meneja Masoko na Mawasiliano huyo wa benki hiyo, alisema kuwa pia benki yao wanatoa unafuu na urahisi wa kupata mikopo na huduma nyingine kadhaa ambazo ziliwafanya watu waliotembelea banda lake kwenye maonyesho ya Sabasaba lililopo ukumbi wa Karume, upande wa kulia wa lango la kuingilia kuhamasika na kutaka kujua zaidi kuhusu benki hiyo. “I&M inafungua milango kwa Watanzania wote kwenda kujiunga na benki inayojali mahitaji yao, iliyo tayari kuwapa huduma za kipekee za kifedha kupitia wafanyakazi wake wenye uzoefu zaidi katika kutoa huduma bora kwa wateja. “Mbali na kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba, benki hiyo inatoa huduma zake bora kupitia mtandao wa matawi yake yaliyoko maeneo ya Maktaba, Indira Gandhi, Nyerere, Kariakoo, Oysterbay pamoja na mikoani ikiwa ni pamoja na Moshi, Arusha na Mwanza,” alisema Timu ya wafanyakazi wa mauzo na idara ya masoko wa benki hiyo kutoka matawi yake ya Dar es Salaam inayoongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wapo kwenye maonyesho hayo ili kuwapa wageni na wale ambao wanataka kuwekeza katika benki inayoaminika na salama ikiwa na huduma za ATM zinazopatikana kwa saa 24. | 5 |
Derick Milton -Simiyu IKIWA ni takribani mwezi mmoja tangu Januari 9,
Baraza la Mitihani (NECTA), lilipotangaza matokeo ya kidato cha nne na Yohana
Lameck (19) kuibuka shujaa wa shule za kata kwa ufaulu wa A tisa licha mazira
magum aliyokuwa nayo, baba yake aliyeikimbia familia kwa miaka saba, ameibukia
kwenye hafla ya kumpongeza. Yohana aliyekuwa akisoma shule hiyo ya kata
iliyopo wilayani Bariadi Mkoa wa Simiyu, kwa miaka saba alikuwa akiishi na mama
yake huku wakiwa na maisha magumu ambapo wakati mwingine, alilazimika kuacha
shule na kufanya kazi za vibarua za kulima, kuchunga ngombe ama kusukuma
mikokoteni ili aweze kupata chakula. Walimu wake wa shule ya msingi, ndio waliompeleka
shule ya sekondari baada ya kumuona mtaani licha ya kwamba amefaulu na
alipokuwa sekondari, kuna wakati aliacha shule kwa miezi mitatu baada ya kukosa
mahitaji muhimu ikabidi walimu wake wamsake na kumrudisha shuleni na kumpa
mahitaji kama sare na chakula. Katika shule aliyosoma Yohana wanafunzi
waliofanya mtihani huo walikuwa 88 ambapo
yeye pekee ndiye aliyepata daraja la kwanza. Waliopata daraja la pili ni wanne, daraja la tatu
15, daraja la nne 54 na sifuri 13 huku shule yake ikishika nafasi ya 79 kati ya
shule 100 kwenye mkoa na nafasi ya 1991 kati ya shule 3908 kitaifa. Kwa mujibu wa matokeo hayo masomo aliyofanya Yohana
na ufaulu wake kwenye mabano ni Civics (A)
Historia (A), Jographia (A) Kiswahili (A) Kingereza (A) Phizikia (A)
Kemia (A) Bayolojia (A) na Hisabati (A). Baba aibuka Juzi Mkoa wa Simiyu, ulifanya hafala ya kupongeza
wanafunzi waliofaulu mtihani huo ambapo Lameck Lugedenga baba mzazi wa Yohana
aliibuka na kufanya minong’ono kuibuka ukumbini. Aliwasili ukumbini hapo akiwa ameambatana na mke
wake Mariamu Lulyalya pamoja na Yohana. Baada ya kutambulishwa kuwa ndiye baba mzazi wa
Yohana, kulizuka gumzo na minong’ono ukumbini kwani taarifa za kutelekeza
familia kwa miaka saba zilikuwa zinajulikana badaa ya kuandika na vyombo vya
habari. Lugedenga alimuacha
Yohana akiwa darasa la nne Shule ya Msingi Igaganulwa, kutokana na umaskini na
ilidaiwa alikimbilia mkoani Morogoro. Akiongea na Mtanzania mara baada ya kumalizika
kwa hafla hiyo, Lugedenga alisema ni kweli alikiimbia familia yake, kutokana na
kuchanganyikiwa mara baada ya kifo cha mtoto wake wa kike Magreth aliyefariki
dunia mwaka 2011. Alisema Magreth alikuwa mmoja wa wanafunzi wenye
uwezo mkubwa shuleni kumzidi Yohana, lakini baada ya kuugua kwa muda mfupi na
kulazwa Hosptali ya Wilaya Bariadi (Somanda) alipoteza maisha. “Marehemu alikuwa na uwezo mkubwa darasani, lakini
alipoteza maisha zikiwa zimebaki siku mbili afanye mtihani wake wa kuhitimu
darasa la saba, baada ya hapo nilichanganyika nikaamua kuondoka maana nilikata
tamaa,” alisema Lugedenga. Alisema mbali na hilo, ugumu wa maisha ulimfanya
akate tamaa zaidi na kuamua kuondoka nyumbani kwake kwenda mkoani Morogoro kwa
wazazi wake ambao walihamia huko muda mrefu. “Niliunganisha vitu vyote hivyo nikaona niondoke,
maana sina msaada na sina uwezo wa kuisadia familia yangu ni bora kuondoka
nikatufute maisha sehemu nyingine,” alisema Lugedenga Alisema mawasiliano na familia yake yalikuwepo
ingawa kwa kiasi kidogo sana, kwani hata huko alipohamia hakuweza kufanikiwa
kimaisha kutokana na kuendelea kupata matatizo ikiwemo kupoteza wazazi wake
wote. Aisema hakuwa na uwezo tena wa kuisadia familia
yake na taarifa za mtoto wake Yohana kutaka kuacha shule alizipata, lakini
alimsihi asiache bali awe mvumilivu kwani na yeye hana huwezo wa kumsaidia. Aomba radhi Lugedenga aliwaomba radhi mke wake na mtoto wake,
kwa alichowafanyia na kusema hawezi kurudia tena na imekuwa fundisho kwake. Alisema mtoto wake Yohana kufanya vizuri kwenye
mtihani, kimefanya familia yake kuungana tena kwa mara nyingine na kamwe hawezi
kurudia tena kuitelekeza. “Nimejifunza siyo vizuri kuitelekeza familia hata
kama ni shida, lazima uvumilie upambane nazo ukiwa na familia yako, nakiri
nilikosena na ninashukuru mke wangu amenipokea tuendelee na maisha,” alisema
Lugedenga. Lugedenga alisema kwa kwa sasa hawezi tena kurudi
Morogoro, bali ataanza maisha mapya na mke wake na mtoto wake licha ya kuwa
hana uwezo atapamba kuhakikisha anahudumia familia yake. “Nimekuja moja kwa moja siwezi tena kurudi Morogoro,
bado maisha yangu ni magumu lakini nitapambana hivyo hivyo na mke wangu tuweze
kuishi kama zamani,” alisema Lugedenga Alisema kwa sasa anajisikia mwenye nguvu kutokana
na alichokifanya mtoto wake, huku akiwashukuru walimu na wananchi ambao
walimsaidia Yohana kupata mafanikio hayo. Lugedenga alisema licha ya kuishi Morogoro kwa
muda mrefu hajawahi kuwa na familia nyingine, bali alikuwa akiishi na wazazi
wake na kujishughuliza na kilimo hivyo hana mke wala mtoto mwingine. Mke anena Mariamu Lulyalya alisema amemsamehe mme wake,
kwani anajisikia mwenye furaha kuweza kuungana tena naye baada ya kuwakimbia kwa miaka saba. Lulyalya anasema licha ya kutendewa mambo yote na
mme wake, na kuachiwa mzigo wa kulea watoto, hawezi kumkataa kwani ndiye mme
wake halali na wamefanikiwa kupata watoto watano. “Leo najisikia mwenye nguvu sana, nashukuru mme
wangu amerudi na tuko pamoja, alikuja nikampokea maana ni mme wangu na
nimesamehe ili tuweze kuendeea na maisha,” alisema Lulyalya. Yohana. Yohana alisema kitendo cha baba yake kurudi nyumbani
kumempa nguvu na anajisikia mwenye furaha kutokana na kukosa malezi yake kwa
muda. “Ni kweli mimi ni shujaa, bila mimi nahisi Baba
asingerudi nyumbani, lakini kutokana na hiki ambacho nilikifanya leo amerudi,
najisiki mwenye furaha sana, kama mtoto nilikuwa najisikia vibaya kukosa malezi
ya baba,” alisema Yohana. Mkuu wa Mkoa. Awali Mkuu wa Mkoa huo, Antony Mtaka, alimtaka
mzazi wa Yohana kuwa karibu na familia yake na kuhakikisha anamsaidia Yohana
afike mbele zaidi ili aje kuwa msaada kwake. Mtaka alimtaka Lugedenga kuhakikisha anashikamana
na mtoto wake ikiwemo kuwasimamia wadogo zake kuhakikisha wanapata elimu, ili
wawe msaada kwake na mke wake. Akizungumzia matokeo ya kidato cha nne, Mtaka
alisema mkoa kushika nafasi ya tano ndiyo lilikuwa lengo. Aliwashukuru wadau wote wakiwemo wazazi, walimu
na viongozi kwa kusaidia kufikia malengo hayo, huku akibainisha kuwa wataweka
mikakati mipya kuhakikisha mkoa unashika nafasi tatu za juu. | 3 |
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imebuni kifaa cha pikipiki kinachobaini dereva anapobeba watu wengi maarufu kama mishikaki, kulewa au kutovaa kofia za helmeti kwa kuwa pikipiki hiyo haiwaki.Uwezo huo unatokana na pikipiki hiyo iliyobuniwa kufungiwa kifaa maaalum aina ya GPS kwa ajili ya usalama iwapo barabarani.Kutokana na hatua hiyo, Veta imepata ufadhili wa Sh milioni 15 kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) ili kuendeleza pikipiki hizo.Kifaa cha GPS kilichofungwa katika pikipiki hiyo pia kinaweza kutumiwa na dereva kutoa taarifa kwa wenzake kwa alama maarufu pale inapotokea amevamiwa na majambazi au kupata dharura yoyote inayohitaji msaada.Akizungumza katika banda la VETA kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), Msimamizi wa Uvumbuzi wa Chuo cha VETA Kipawa, Charles Mapuri alisema baada ya uvumbuzi wa pikipiki hiyo yenye usalama mkubwa wamepata fedha hizo ili kuendeleza ubunifu.Alisema ubunifu huo uliofanywa na Mwalimu wa masuala ya umeme, Anneth Mganga haiwaki kabisa endapo dereva hajavaa kofia ya helmeti na pia imewekewa Panick Button ambayo ndiyo inayobonyezwa ili kutoa ujumbe dereva anapovamiwa au kupata ajali na kuhitaji msaada wa wenzake ambao atawaunganisha katika kifaa hicho.Mapuri alisema fedha hizo walizopatiwa na Costech zitawawezesha kuongeza ubunifu, na kufanya majaribio ili iwe bora zaidi.Alisema pia wanaangalia nishati itakayotumika kama ni umeme jua au betri kwa lengo la kuboresha na kurahisisha ufanyaji kazi katika mfumo wake mzima.Mwaka jana, ubunifu wa pikipiki hiyo ulikuwepo katika viwanja vya Sabasaba kwa mara ya kwanza na kuvutia watu wengi wakiwemo viongozi wa vyombo vya usalama barabarani na walitaka iongezewe ubora ili iweze kuanza kutumika kwa jamii. | 3 |
JANA katika Kituo cha mabasi cha Nanenane jijini Mbeya kuzilizuka ilikuwa kituko cha aina yake baada ya mkuu wa mkoa, Albert Chalamila kufanya ziara ya kushitukiza kituoni hapo na kisha msafara wake wote kuingia kula chakula katika moja ya migahawa iliyopo kituoni hapo.Hata hivyo, kazi ya wajumbe wa msafara kupata chakula wakiongozwa na mkuu wa mkoa haikuwa ndogo kwani muda mfupi tu baada ya waliokuwa kwenye msafara kuketi wakisubiri huduma katika mgahawa uliofahamika kwa jina la Bisamia, kundi kubwa la wapigadebe na wamachinga walivamia wakitaka kula chakula na vinywaji pamoja na mkuu wao wa mkoa.Msafara wa Chalamila uliwasili kwenye kituo hicho cha mabasi majira ya saa nane kasorobo na baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa vibanda 16 vinavyojengwa kwa ajili ya kupumzikia abiria msafara ulielekea kwenye vibanda kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ambavyo hadi sasa halmashauri ya jiji inawashawishi wafanyabiashara kuhamia. Baada ya ukaguzi huo, Chalamila aliamuru msafara wote kwenda kwenye vibanda vya mamalishe ili kuwaunga mkono kwa kununua chakula na ndipo msafara ukaelekea kwenye vibanda vilivyopo pembezoni kwa kituo hicho cha mabasi na kuagiza chakula kabla ya wapigadebe, makondakta, madereva na machinga kufika.Hata hivyo licha ya wauzaji chakula na vinywaji baridi kuonekana kuelemewa na umati uliofurika huku baadhi ya watu wakisukumana ili kulazimisha kupata huduma, wengi wa waliofika walipata chakula na vinywaji hatua iliyofurahiwa na kila aliyefika. Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya waliofika wakiwemo wafanyabiashara wa vyakula walimpongeza Chalamila kwa hatua hiyo wakisema ameonesha uongozi wa kushirikiana katika shida na raha hadi na watu wa chini kabisa.“Hawa ndiyo viongozi tunaowataka... ndiyoooo ....siyo kiongozi anayekaa ofisini kila siku hajui hata watu wanakula nini huku mitaanii.... Ndiyoooo,”zilisikika sauti za shangwe zikisema huku wakizidi kusema Chalamila hoyeee na wengine wakisema Chalamila safiii!!. Akizungumza na wadau katika kituo hicho, mkuu huyo wa mkoa aliwaahidi kuendelea kuboresha mazingira ya stendi hiyo ili abiria wasipate usumbufu wa aina yoyote wawapo kituoni wakisubiri usafiri au wanapofika. | 3 |
KHABAROVSK, URUSI MAELFU ya waandamanaji wamemiminika katika mitaa ya mji wa Mashariki ya mbali ya Urusi wa Khabarovsk, wakipinga kukamatwa kwa gavana wa mkoa huo, kutokana na tuhuma za kuhusika katika mauaji. Vyombo vya habari vya ndani vimekadiria kuwa kiasi ya waandamanaji 50,000 wameshiriki maandamano hayo yaliyofanyika jana. Maandamano hayo yamefanyika kila siku ndani ya wiki hii, ambapo mamia ya watu walikusanyika katikati ya mji, na kuashiria hasira kubwa juu ya kukamatwa kwa gavana na kutoridhika na sera za serikali ya Urusi. Sergei Furgal, gavana maarufu wa Khabarovsk alikamatwa wiki mbili zilizopita na kusafirishwa hadi Moscow na kuwekwa jela kwa muda wa miezi miwili. Anatuhumiwa kushiriki kwenye mauaji kadhaa ya wafanyabiashara kati ya mwaka 2004 na 2005 kabla ya kuanza safari yake ya kisiasa. Wakati huo huo Ripoti mpya ya wizara ya ulinzi ya Marekani Pentagon, imeeleza kuwa Uturuki iliwatuma kiasi ya wapiganaji 3,500 hadi 3,800 wa Syria nchini Libya katika kipindi cha miezi miwili ya kwanza ya mwaka huu. Ripoti hiyo imetolewa wakati mgogoro katika taifa hilo lenye utajiri wa mafuta Libya, ukizidi kuongezeka katika vita vya mataifa ya kigeni nchini humo yanayoingiza silaha na wapiganaji katika taifa hilo. Jeshi la Marekani lina wasiwasi na ongezeko la ushawishi wa Urusi nchini Libya, ambako mamia ya wapiganaji wa kirusi wanaunga mkono kampeni ya kuutwaa mji mkuu wa Tripoli. Ripoti hiyo ya robo mwaka kuhusu operesheni za kukabiliana na ugaidi barani Afrika, inasema Uturuki iliwalipa na kutoa uraia kwa maelfu ya wapiganaji kuungana na wapiganaji wa serikali ya Tripoli dhidi ya vikosi vya kamanda Khalifa Haftar. | 2 |
BAJETI Kuu imeleta kicheko kwa makundi mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara ambapo serikali imetoa misamaha, imepunguza kodi na kufuta tozo mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwa taasisi mbalimbali za serikali zilizokuwa zikiathiri mazingira bora ya biashara.Aidha kupitia bajeti hiyo, serikali imepiga marufuku Mamlaka ya Mapato (TRA) kuwafungia biashara kushinikiza kulipa kodi au malimbikizo isipokuwa kwa kibali cha Kamishna Mkuu wa mamlaka.Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk Philip Mpango aliwahakikisha wafanyabiashara kwamba katika mwaka ujao wa fedha serikali itatekeleza mpango kazi wa uwezeshaji mazingira ya biashara mazingira yawe rafiki na yenye gharama zaidi.Alisema serikali itaimarisha ukusanyaji wa mapato ya kodi bila kuathiri biashara.“Nawaagiza TRA hairuhusiwi kufunga biashara ili kushinikiza mfanya biashara alipe kodi au malimbikizo ya kodi isipokuwa kwa kibali cha kamishna mkuu wa mamlaka ya kodi,” alisema.Vile vile kuanzia mwaka ujao wa fedha unaoanza Julai mwaka huu, wananchi wa kawaida wataruhusiwa kuchukua mizigo bandarini bila kuwa na ulazima wa kutumia wakala wa forodha. Utaratibu huu hautahusisha mizigo inayopita nchini kwenda nje.Tozo, ada zafutwaMiongoni mwa taasisi ambazo zimefutiwa tozo ni Shirika la Viwango (TBS) ambalo kuanzia mwaka ujao wa fedha, hakutakuwa na tozo ya Sh 50,000 ya maombi ya alama ya ubora; gharama za mwanzo za ukaguzi wa ubora; dhamana ya cheti cha kutumia nembo ya ubora na tozo ya ununuzi wa fomu ya ununuzi wa bidhaa zinazotoka nje kwa bidhaa zote.Nyingine ni tozo ya gharama za ujenzi ambayo hutozwa kwa gharama ya ujenzi.Aidha, kuanzia mwaka ujao wa fedha, TBS itaendelea kusimamia vipodozi na chakula kama ilivyokuwa mwaka 1975.Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) itaendelea kusimamia vifaa tiba na tendanishi. Taasisi nyingine ambazo tozo zake zimefutwa ni pamoja na Mkemia Mkuu wa Serikali; Sekta ya mifugo na maliasili na utalii.Ada nyingine zilizofutwa ni ya matumizi ya maji kwa wenye visima vya maji lengo likiwa ni kupunguza gharama kwa wananchi wanaochimba visima majumbani kwa ajili ya matumizi yao. Ili kudhibiti uchimbaji holela, itabidi viendelee kusajiliwa.Miongoni mwa maeneo ambayo yamepunguziwa kodi ni pamoja na umeme unaouzwa kutoka Bara kwenda Zanzibar ambao VAT imepunguzwa kutoka asilimia 18 hadi 0 . | 5 |
ILE adha ya mafuriko katika Mto Msimbazi jijini Dar es Salaam, inayosababisha daraja la Jangwani kufunikwa na maji imepatiwa ufumbuzi.Wakati wowote kuanzia sasa, daraja hilo litafumuliwa na kujengwa upya kwa kunyanyuliwa mita 300.Hayo yalielezwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda wakati akizungumza kwenye kongamano maalumu kuelekea uchaguzi, uchumi wa viwanda, amani, mahusiano, uzalendo na ustawi wa Taifa lililoandaliwa na Kamati ya Amani mkoani humo.Makonda alisema; “ninaomba radhi ya kuchelewa kuhudhuria kongamano hili kwa wakati, nilikuwa nifuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani kwangu, na niwaeleze tu katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inatelekezwa, tumepata fedha Dola za Marekani milioni 120 kwa ajili ya kukabiliana na changamoto ya mafuriko Bonde la Msimbazi, tunafumua Daraja la Jangwani na kulinyanyua kwa mita 300.”Alisema fedha hizo zimepatikana kutoka Benki ya Dunia za kuijenga upya Jangwani. Tayari upembuzi yakinifu umefanyika ili kumaliza changamoto ya mvua na mafuriko eneo hilo, yanayosababisha mawasiliano kuvunjika.“Lengo ni kumaliza changamoto kubwa tulizozoea kuziona hasa kwenye bonde hilo la Msimbazi lakini kubwa katika daraja hilo la Jangwani…sasa tunalinyanyua mita 300 na kila upande tunatengeneza maeneo ya kutalii na kujenga hoteli na pia tutaweka boti za utalii katika mto huo ili wanaopenda kuona mto huo kuelekea baharini wafanya utalii wao,” alisema Makonda.Alisema baada ya kunyanyua daraja hilo, maji yatapita kwa urahisi na kwa kasi kuelekea baharini.Kwamba mtaalamu mshauri kwenye upembuzi yanikifu, alichora michoro itakayotumika kunyanyua daraja hilo ili pia kuruhusu boti kupita chini yake na maji mengi nayo kusafiri bila kikwazo.Akizungumza kujengwa upya kwa barabara kuanzia Buguruni hadi kuunganisha na barabara ya Morogoro, kuelekea kwenye daraja hilo yenye umbali wa kilometa nane, Makonda alisema njia hiyo inafumuliwa na kujengwa upya na kwamba ujenzi huo utaanza muda wowote kuanzia sasa.Awali, akitoa mada kuhusu uhusiano wa kufanya kazi kwa bidii na ustawi wa Taifa kwenye kongamano hilo, Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe alisema Tanzania ina bahati ya kumpata Rais John Magufuli anayehimiza wananchi kufanya kazi.“Tanzania tuna bahati ya kumpata Rais anayehimiza watu wake kufanya kazi, yeye mwenyewe ni mchapakazi na kauli yake ya ‘Hapa Kazi Tu’ ni nzito isichukuliwe kimzaha na kama tukimpa muda zaidi Rais Magufuli atatufundisha kufanya kazi zaidi kwa manufaa yetu,” alisema Askofu Kakobe.Akitoa salamu zake, Mufti wa Tanzania, Abubakari Zubeir alisema viongozi wa dini wana jukumu la kusimamia uzalendo na kuhimiza waumini wao kufanya matendo ya amani ili nchi iwe na maendeleo ya kweli.“Viongozi wa dini tuna wajibu mkubwa wa kuwahimiza na sisi pia kuwa mfano wa kuwa wazalendo na kuhimiza amani kwani ni alama dhahiri ya mtu aliyeshika dini, tunapoelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao tuhakikishe tunahimiza waumini wetu kushiriki kwenye uchaguzi huo na kuchagua viongozi sahihi kwa maslahi ya maendeleo yetu,” alisema Mufti Zubeir.Aliongeza nchi haina dini ila watu wake wana dini na kinachoongoza nchi ni Katiba ambayo imeweka bayana jinsi ya kupata viongozi kwa kufanya uchaguzi, ambao wananchi wake wanapaswa kushiriki kikamilifu ili kupata viongozi waadilifu watakaoshirikiana na wananchi kuleta maendeleo.Akisoma hotuba ya ufunguzi ya mgeni rasmi, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara alisema mchango wa taasisi na madhehebu ya dini katika kujenga ustawi wa watu na nchi, umechangia maendeleo nchini. | 3 |
KOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger, amemmwagia sifa mshambuliaji wake, Alexis Sanchez, kutokana na kiwango alichokionesha kwenye mchezo wa mwishoni mwa wiki dhidi ya West Ham. Katika mchezo huo, Arsenal ilifanikiwa kushinda mabao 5-1, huku mshambuliaji huyo akiweka historia yake kwa kufunga mabao matatu (hat trick) ndani ya dakika 14, hivyo kuzidi kumchanganya kocha huyo. Katika mchezo huo ambao ulikusanya watazamaji 56980 huku West Ham wakiwa kwenye uwanja wa nyumbani, walijikuta mashabiki wao wakitoka uwanjani mmoja mmoja baada ya kichapo hicho katika dakika za lala salama. Wenger ameweka wazi katika ulimwengu huu wa soka kuwa washambuliaji bora wanaofanya vizuri duniani wanatoka America Kusini, hivyo kati ya washambuliaji hao ni pamoja na mchezaji wake Sanchez. “Sanchez anazidi kuonesha ubora wake katika soka, katika ushindi wetu wa mabao matano, ametoa mchango mkubwa, hapa ni sehemu yake sahihi na ndio maana anaonesha kiwango cha hali ya juu. “Ameweza kuweka historia mpya ya kutumia dakika 14 kufunga mabao matatu, huku ikiwa ni mara yake ya pili kupachika mabao matatu katika ligi tangu ajiunge na klabu hii. “Mchango wake ni mkubwa ndani ya klabu, kama atacheza chini ya kiwango basi timu hiyo itakuwa katika wakati mgumu na kama akiamua kucheza katika kiwango chake, basi inakuwa kazi rahisi kwa wachezaji wengine kuonesha uwezo wao,” alisema Wenger. Kocha huyo mbali na ushindi alioupata, lakini amekisifia kiwango ambacho West Ham walikionesha ndani ya dakika 90. “Ni wazi tumecheza na timu bora sana katika ligi kuu, wameonesha kupambana kwa dakika 90, lakini kitu ambacho tutaendelea kujilaumu ni kwamba tumeshindwa kutumia nafasi nyingi katika dakika 45 za kipindi cha kwanza, ninaamini kama tungeweza kufanya hivyo basi tungekuwa na mabao mengi zaidi. “Lakini kwa kuwa wachezaji wangu walishindwa kufanya hivyo katika kipindi cha kwanza, basi waliweza kupambana kwa ajili ya kipindi cha pili na waliweza kutumia nafasi walizozipata,” aliongeza. Kwa upande wa kocha wa klabu ya West Ham, Slaven Bilic, amedai kuwa amepoteza mchezo huo mbele ya timu bora na walishindwa kuzitumia nafasi walizozipata. “Ninaamini tunaweza kufanya vizuri msimu huu kama ilivyo msimu uliopita, lakini hatuwezi kushinda katika kila mchezo, kuna wakati tunaweza kufanya vizuri na wakati mwingine tunapoteza, lakini bado tuna nafasi ya kuendelea kufanya vizuri. “Kwa matokeo haya, naomba nitumie nafasi hii kuomba radhi kwa mashabiki wa klabu hii pamoja na wadau wa soka kutokana na matokeo mabaya tuliyoyapata, ni wazi kuwa ni mabaya. “Tupo katika kipindi kigumu hasa katika kushuka daraja, lakini ninaamini wachezaji wote wanalijua hilo na wanapambana kuhakikisha tunabaki kwenye ligi,” alisema kocha huyo. | 4 |
WAKALA wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) umefanikiwa kununua magari 599 kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2019 na kuokoa zaidi ya Sh bilioni 4.7 kupitia ununuzi wa pamoja.Ofisa Mtendaji Mkuu wa GPSA, Dk Geraldine Rasheli, alitoa takwimu hizo mjini hapa juzi na kusema kuwa ununuzi wa magari hayo 599 uligarimu Sh bilioni 96.7.“Kupitia ununuzi wa pamoja wa magari ya serikali 599 kutoka taasisi za umma 242, tumepunguza gharama kwa Sh bilioni 4.71 endapo kila taasisi ingenunua yenyewe,” alisema.Dk Rasheli alisema kutokana na ununuzi huo, Sh bilioni 1.5 zimeokolewa katika mchakato wa manunuzi na Sh bilioni 3.147 zimeokolewa kutokana na punguzo linalotolewa kutokana na ununuzi wa pamoja.“Kati ya fedha zilizokolewa, Sh bilioni 1.5 zimeokolewa katika mchakato wa manunuzi, kama taasisi 242 zingefanya machakato wa manunuzi zenyewe, inakadiliwa kila taasisi ingetumia Sh milioni 6.5,” alisema.Alisema pia GPSA ambayo imekuwa ikitoa huduma ya ugomboaji wa mizigo mikubwa ya serikali, imefanya kuwapo kwa ongezeko la thamani ya mizigo inayogombolewa ambayo imeongezeka kutoka thamani ya mizigo ya Sh bilioni 40.358 kwa mwaka 2017/18 hadi kufikia mizigo yenye thamani ya Sh bilioni 68.139 kwa wastani kwa mwezi kwa mwaka wa fedha 2018/19.“Kuanzia Julai mwaka 2019 hadi Desemba mwaka jana, thamani ya mizigo yenye thamani ya Sh milioni 700 iligombolewa, hivyo kuongezeka kwa thamani ya mizigo kumeongeza pato la wakala katika sehemu hii kutoka wastani wa Sh milioni 200 kwa mwaka mpaka kufikia Sh milioni 150 kwa mwezi kwa mwaka 2019/2020,” alisema.Alisema upungufu wa watumishi umechangia kutofanya vizuri zaidi kwenye eneo la ugomboaji wa mzigo na kuwa wamekuwa wakishirikiana na Wizara ya Kazi na programu ya kuboresha vijana katika ajira ili kutoa mafunzo kwa vitendo kwa vijana sehemu ya ugomboaji na imekuwa fursa ya kuwatumia vijana hao katika kutoa huduma.Aidha, Rasheli alisema kwa mwaka wa fedha 2020/21 wakala umepanga kukusanya Sh bilioni 79.1 kupitia vyanzo vyake vya mapato, ambapo Sh bilioni 16.163 zinatarajiwa kuwa ni faida kutokana na makusanyo na ruzuku serikalini kama mishahara. | 3 |
Na Bakari Kimwanga-DAR ES SALAAM
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba, amevunja ukimya na kusema amepokea adhabu aliyopewa na chama chake kwa moyo mkunjufu.
Kutokana na hali hiyo, amesema hana mpango wa kujiunga na chama chochote cha siasa, kwani ataendelea kubaki kuwa mkereketwa wa chama hicho tawala.
Sophia alitoa kauli hiyo jana katika mahojiano maalumu na MTANZANIA yaliyofanyika nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.
Alisema kwa takribani miaka 46 amekuwa mwanachama mwaminifu wa CCM, hivyo haoni sababu ya kukiacha chama hicho.
Akizungumza kwa kujiamini, Sofia alisema alijiunga na Chama cha TANU mwaka 1971, wakati huo akiwa Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na Katibu wa UWT Tawi la NDC nafasi ambayo alidumu nayo hadi mwaka 1979.
Baadaye mwaka 1977 alijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuzaliwa kwake.
Adhabu dhidi yake
MTANZANIA ilipotaka kujua namna alivyopokea adhabu hiyo na majaliwa yake ya baadaye, Sophia alisema amepokea uamuzi huo kwa mikono miwili kwani adhabu aliyopewa ni halali kwake, ingawa katika maisha yake ya kisiasa hakuwahi kukisaliti chama chake.
“Kwanza una bahati msimamo wangu ni kutozungumza na waandishi wa habari ila kwa kuwa ni wewe haya… Kuhusu adhabu ya chama binafsi nimeipokea kwa mikono miwili na sina kinyongo na uamuzi wa chama changu hata kidogo.
“Ninajua wapo waliozusha, eti baada ya uamuzi wa Dodoma nimekwenda kukutana na mwanasiasa mmoja wa upinzani, taarifa hizi si za kweli na sitofanya hivyo. Nimetoka Dodoma na kurejea hapa nyumbani kwangu Dar es Salaam nimepokewa na watoto wangu, ndugu na marafiki zangu.
“Napenda kuwaeleza Watanzania wote, wafahamu sina mpango wa kujiunga na chama chochote cha upinzani. Na unajua CCM ina makundi mawili, la kwanza ni wanachama wenye kadi na la pili wakereketwa ambao ni wengi nami nitaingia katika kundi hilo na si kuhama,” alisema Sophia.
Alisema kwa miaka yake ya sasa, ikiwamo uzee hana muda wa kuhangaika katika vyama kwa sababu ujana wake wote ameumalizia ndani ya CCM.
Kwenda mahakamani
MTANZANIA ilipomuuliza kama ana mpango wowote wa kwenda mahakamani kupigania uanachama wake kupinga adhabu aliyopewa, Sophia alisema hana mpango wa kwenda mahakamani kwa sababu kila taasisi huwa na utaratibu wake na si vinginevyo.
“Moyo wangu, maisha yangu yote ya ujana nimetokana na CCM, suala la kwenda mahakamani kupinga uamuzi wa chama kwangu halipo na sina nia hiyo hata kidogo, chama kupitia mwenyekiti wetu, Rais Dk. John Magufuli kimechukua hatua kwa wema na fadhila zote nilizopewa bado niende mahakamani?
“… nasema tena hili kwangu hapana sitofanya hivyo unaweza kwenda mahakamani halafu iwe nini, maisha yangu yote yametokana na CCM na leo kwenda mahakamani ni kukosa fadhila nilizozipata ndani ya chama.
“Kama suala ni ubunge wa viti maalumu kinachopanga nani awe mbunge ni chama ambacho pia kinaweza kusema hapana …msimamo wangu naheshimu uamuzi halali ya chama,” alisema Sophia.
Alisema pamoja na mtihani uliomkuta bado ataendelea kuenzi na kutambua mchango mkubwa wa chama hicho katika maisha yake yote ya ujana hadi utu uzima kwa sasa.
Ajivunia marais watatu
Alisema kutokana na uwezo aliopewa na Mwenyezi mungu, amepata bahati ya kufanyakazi na marais watatu kwa nyakati tofauti ambapo kila mmoja amefanya kazi nzuri ya kukijenga CCM.
“Usipoweza kumshukuru Mwenyezimungu huwezi kumshukuru yeyote, mwanangu mimi nina bahati ya pekee nimejaaliwa kufanyakazi kwa karibu na marais watatu, Rais mstaafu Benjamin Mkapa kama mbunge.
“… na si hivyo tu kufikia mwaka 2005 hadi 2015 nimefanyakazi na Rais mstaafu Jakaya Kikwete na mwaka 2015 hadi sasa 2017, nimefanyakazi na mwenyekiti wetu wa chama, Rais Magufuli ambao wote kwa nyakati tofauti, wamekuwa viongozi wangu,” alisema.
Sophia, alisema wakati wote anamshukuru Mungu kwa kumjalia neema hiyo ya kufanyakazi na viongozi hao ambao wakati wote walikuwa msaada kwake.
Usaliti
Alisema pamoja na kupewa adhabu ikiwamo kufanya usaliti kwa chama, hivi sasa hawezi zungumzia suala hilo ila nafsi yake imekuwa ikijua ukweli namna alivyo mwaminifu.
“Sitaki kuzungumzia kwa undani suala la usaliti ila kwa kifupi, Mungu anaishuhudia nafsi yake jamani hivi kweli nikisaliti chama changu ambacho kimenilea katika maisha yangu yote.
“Sitaki kusema hili ila kikubwa ninaomba umma na wana CCM wote watambue nimepokea adhabu kwa mikono miwili na sina kinyongo chochote,” alisema.
Mitandao ya kijamii
Aliwaomba Watanzania kuitumia mitandao ya kijamii kwa faida hasi na si vinginevyo, ikiwamo kumwekea maneno mdomoni.
“Ninawaomba Watanzania wenzangu tuitumia mitandao ya kijamii kwa faida maana hivi sasa kila jambo limekuwa likizushwa ikiwemo kuwekewa maneno kinywani si jambo zuri ndugu zangu,” alisema.
Nafasi alizoshika
Sophia Simba, amekuwa Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto sambamba na kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ambapo kwa nafasi yake pia, alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC).
Waliofukuzwa
Machi 11, mwaka huu, CCM ilitangaza kuwafukuza wanachama wake 12, akiwamo Sophia ambaye wiki iliyopita alitangaza kutogombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi wa ndani ya chama hicho unaofanyika mwaka huu.
Wengine ni wenyeviti wa mikoa ambao ni Jesca Msambatavangu (Iringa), Erasto Kwilasa (Shinyanga), Ramadhan Madabiba (Dar es Salaam) na Christopher Sanya (Mara).
Wengine ni Willfred ole Mollel ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Mjini, mjumbe wa NEC wa Wilaya ya Babati Mjini, Ally Sumaye na Mathias Manga wa Wilaya ya Arumeru.
Katika orodha hiyo, pia wamo wenyeviti wa wilaya ambao ni Omari Awadhi (Gairo), Ally Msuya (Babati Mjini), Makolo Laizer (Longido) na Salumu Madenge (Kinondoni-Dar es Salaam).
Wanachama wengine waliochukuliwa hatua baada ya kufanya makosa kama hayo ni Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi ambaye amepewa onyo kali na anatakiwa kuomba radhi.
Wakati Nchimbi akipewa onyo hilo, Adam Kimbisa ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma na Mbunge wa Afrika Mashariki alisamehewa. | 1 |
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mbeya imewahukumu kunyongwa hadi kufa watu wanne kutoka wilayani Mbozi mkoani Songwe, baada ya watatu kati yao kukutwa na hatia ya kuua kwa kukusudia ili kuiba Sh milioni moja ;na mmoja kuua na kuchukua viungo vya sehemu za siri za marehemu na kupeleka kwa mganga wa kienyeji. Katika hukumu ya kwanza, mahakama hiyo imemhukumu kunyongwa hadi kufa, Aman Kalinga (23), mkazi wa Kijiji cha Mpanda Kata ya Nyimbili kwa kumuua Heroni Kalinga (13) na kuchukua viungo vyake vya siri na kupeleka kwa mganga wa kienyeji, aliyefahamika kwa jina moja la Makamu.Katika hukumu ya pili, Nathan Elias, Moses Kasitu na Elias Mzumbwe wakazi wa wilayani Mbozi, walitiwa hatiani na mahakama hiyo kwa kushiriki kumuua Vasko Njowela, aliyekuwa akifanya kazi ya kuuza duka katika eneo la Mpemba Tunduma wilayani Momba na kupora Sh milioni moja. Tukio hilo lilitokea saa 1:30 usiku Julai 25 mwaka 2014 wakati muuza duka huyo akiwa getini kuingia nyumbani kwa mwajiri wake. Hakimu wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Dk Adam Mambi alisema kitendo hicho ni kinyume cha kifungu cha sheria. Akitoa hukumu, alisema mahakama imejiridhisha pasipo kuacha shaka yoyote kufuatia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, kuwa watu hao walitenda kosa hilo la mauaji. Alisema imethibitika kuwa watuhumiwa walimvamia Njowela wakati akiingia getini nyumbani kwa bosi wake akitoka dukani, wakiwa na lengo la kumpora begi ambalo aliweka fedha hizo. Alisema mara baada ya kumvamia muuza duka huyo, ulizuka ugomvi baina yake na mshitakiwa namba moja Nathan. Mshitakiwa namba mbili, Kasitu aliungana na mshitakiwa namba moja kumshambulia Njowela kisha mshitakiwa namba tatu, Mzumbwe alimpiga muuza duka huyo tumboni kwa bunduki. Alisema mshitakiwa namba moja, Nathan aliendelea kumkata mapanga Njowela, jambo lililosababisha apoteze uhai. Jaji Mambi alisema upande wa mashitaka ulikuwa na mashahidi 10, akiwemo Rehema Saidi aliyekuwepo kwenye eneo la tukio wakati washitakiwa wakifanya mauaji hayo, ambapo aliamuriwa alale chini baada ya washitakiwa kupiga risasi juu huku wakiendelea na mauaji hayo na uporaji wa fedha. Alisema baada ya polisi kuwakamata wahusika wa tukio hilo, shahidi huyo aliwatambua wawili kati yao, ambao ni mshitakiwa namba mbili Kasitu, mkazi wa Kilimahewa na mshitakiawa namba tatu Mzumbwe, mkazi wa Ihanda. Aliwatambua baada ya kupitishwa kwenye gwaride la utambuzi lililowashirikisha watu 12. Alisema ushahidi wa kimaabara, pia ulithibitisha kuwa maganda ya risasi yaliyookotwa eneo la tukio, ndio yaliyotumika katika silaha aliyokamatwa nayo Nathan akiwa Njombe, baada ya washitakiwa wenzake kueleza mahali alipo. Aliongeza pia kuwa maelezo ya awali waliyoyatoa polisi, yanaonesha kuwa washitakiwa hao walikiri kuhusika na tukio hilo na katika matukio mbalimbali katika mkoa wa Songwe. Watu hao walikuwa wakitumia short gun yenye namba 007700112. Waliieleza mahakama kuwa hununua risasi nchini Zambia. | 3 |
KIGALI, RWANDA KATIKA juhudi za kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona, Rwanda imezindua mashine ya kwanza iliyotengenezwa nchini mwake ambayo inawasaidia wagonjwa kupumua maarufu kama ventilator. Ni mashine iliyotengenezwa na vijana wanane wa Chuo Kikuu cha Rwanda kwa msaada wa wakufunzi wao na lengo likiwa ni kuitua Serikali mzigo wa kuagiza mashine kama hizi kutoka nje. Kwa kawaida mashine hii inayomsaidia mgonjwa aliyeko mahututi kupumua wenyewe wanasema thamani yake ni Dola 10,000 za Marekani (karibu Sh. milioni 23.1) inaponunuliwa kutoka nchi za nje. Hata hivyo mabingwa walioitengeneza walisema kwamba kwa sasa kutokana na dunia kukabiliwa na tatizo la Covid-19 bei ya mashine hii imepanda hadi Dola 20,000 za Marekani (karibu Sh. Milioni 46.3). Mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Rwanda, Profesa Stephen Rulisa, alisema licha ya kuongoza mchakato wa kuitengeneza mashine hii ni vijana wake walioitengeneza. “Sisi tunawapa kazi ya kisayansi, tunawapa mawazo kama haya kisha wao hukaa kwenye maabara kama hapa na tunafurahi kwamba hatimaye wanafanya jambo kama hili,” alisema Profesa Rulisa. Wahandisi vijana waliotengeneza mashine hiyo walisema haikuwa kazi ndogo lakini iliwezekana na inawezekana kuzitengeneza nyingine nyingi za aina hiyo, lakini hilo litategemea pale tu serikali itakapowajibika zaidi. “Tunachohitaji ni ushirikiano wa ngazi zote ili tutengeneza mashine nyingi na kuziweka sokoni kwa sababu zinahitajika kwa wingi,” alisema Costa Uwitone, mmoja wa wanafunzi walioshiriki kutengeneza mashine hiyo. Wakati huo huo, pia viwanda nchini Rwanda vimeanza kutengeneza barakoa ambazo Serikali inasema kutokana na hilo, iko mbioni kumtaka kila mwananchi kuiva popote anapokuwa ili kujikinga dhidi ya virusi vya corona. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya tiba, Dk. Nsanzimana Sabin alisema barakoa zina ubora kama zile zinazoingizwa nchini kutoka nje. “Tunatambua bei ya barakoa na ubora wake kwa kuzingatia afya zetu kama binadamu, hatupendi kutengeneza vitu vyenye viwango vya chini hapana, ila barakoa zina viwango bora na pia bei ambayo kila mmoja anaweza kumudu,” alisema. Kwa mara ya kwanza idadi ya wagonjwa wanaopona na kuruhusiwa kutoka nchini Rwanda imepanda kuliko ile ya wagonjwa wanaoendelea kulazwa. | 2 |
BIASHARA ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Afrika kwa ujumla, inatajwa kukua kwa kiwango cha chini ikiliganishwa na kanda nyingine ulimwenguni.Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwanda na Biashara katika Sekretarieti ya SADC, Calicious Tutalife amesema ikilinganishwa na kanda nyingine duniani, biashara iko chini katika SADC na Afrika.Akieleza shughuli za kurugenzi ya maendeleo ya viwanda na biashara kwa waandishi wa habari jana Dar es Salaam, alisema thamani ya biashara ya ndani imeendelea kubaki chini kwa asilimia 22 ya biashara yote ya SADC.Alisema kasoro hiyo ni miongoni mwa zilizobainika kupitia maadhimisho ya wiki ya viwanda yaliyohitimishwa hivi karibuni jambo ambalo ameshauri ifanyike mikakati kuondokana nazo.Akisisitiza jumuiya kuweka kipaumbele cha biashara ndani ya ukanda, alisema pia inapaswa kutatua matatizo ya miundombinu, kupunguza vikwazo, kuboresha ubunifu na utafiti.Amesema baraza jipya la biashara lililozinduliwa, linapaswa kushirikiana na nchi wanachama kuboresha na kuwezesha mazingira ya ushindani kwa kuhusisha ukanda, nchi na sera za ndani kiasi cha kuwezesha kuleta matokeo chanya katika maendeleo ya kiuchumi.Amesema pia uwekezaji katika utafiti, maendeleo na ubunifu umeendelea kubaki chini huku nchi nyingi zikiwekeza chini ya asilimia moja ya pato la ndani (GDP).“Upo umuhimu wa kuboresha mfumo wa elimu ikiwamo teknolojia mpya, kuwekeza kwenye miundombinu ya teknolojia ya habari na mawasiliano, vituo vya umahiri, ubunifu na vituo vya viwanda ili kuongeza fursa za Mapinduzi ya Nne ya Viwanda,” amesema.Alishauri kuwa pia upo umuhimu wa kusaidia fedha za kuanzisha nyenzo za kuunga mkono ubunifu na maendeleo ya teknolojia. | 5 |
Na MWANDISHI WETU SHANGWE za tamasha la Tigo Fiesta zitakuwa zikirindima Tabora leo kwa wakazi wake kupata burudani ya aina yake kutoka kwa wasanii mbalimbali watakaopanda jukwaani. Wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya wamejipanga kutoa burudani ya uhakika katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, ili kuwaridhisha mashabiki wao ambao wana kiu ya kuwaona wakiimba nyimbo kwa kuwashuhudia tofauti na kuwasikiliza redioni au kuwashuhudia kwenye runinga. Wasanii ambao wako mkoani hapa tayari kwa ajili ya kuwapa mashabiki wao burudani katika tamasha hilo la Tigo Fiesta ni pamoja na Chege, Ney wa Mitego, Nandy, Maua Sama, Darassa, Rostam, Mr Blue, Young Dee, Aslay, Jux, Msami na Ben Pol. Wasanii Roma Mkatoliki na Stamina wamekuwa wakiwapagawisha mashabiki wa tamasha hilo kutokana na kuwateka kihisia kupitia wimbo wao wa pamoja uitwao ‘Hivi ama vile’. Pia Chege atakuwa kivutio katika Tigo Fiesta na mashabiki wa muziki wa kizazi kipya watakuwa na shauku ya kutaka kumshuhudia akiimba nyimbo zake mbalimbali, ikiwamo ile mpya ya ‘Runtown’ sambamba na ule wa ‘Kelele za Chura’ aliyomshirikisha mwanadada Nandy, ambaye ni miongoni mwa wasanii watakaokuwapo katika tamasha hilo. Kwa upande wa Ney wa Mitego, anatarajiwa kuwapagawisha wakazi wa Tabora akiwa na wimbo wake wa ‘Wapo’ na nyinginezo. Nandy, ambaye ameonekana kuliteka jukwaa katika Tigo Fiesta tangu ilipozinduliwa jijini Arusha, naye anasubiriwa kwa hamu kutoa burudani akiwa na wimbo wake wa ‘Wasikudanganye’, Nagusagusa na nyinginezo. Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Gwamaka Mwakilembe, alisema mwaka huu wameamua kudhamini Fiesta ili kusaidia vipaji vya wasanii na kuwaletea wateja wao burudani pamoja na kuwapatia vifurushi wanaponunua tiketi za Tigo Fiesta kwa Tigopesa. Kauli mbiu ya Tigo Fiesta mwaka huu ni ‘Tumekusoma’ na kwamba baada ya wasanii hao kuuwasha moto Tabora, burudani hiyo itaendelea katika mikoa Dodoma, Iringa, Songea, Njombe, Sumbawanga, Morogoro, Tanga, Kilimanjaro, Mtwara na kuhitimishwa jijini Dar es Salaam. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tigo Fiesta, Sebastian Maganga, alisema kuwa, Tigo Fiesta ni burudani ya kipekee ndani ya Ukanda wa Afrika Mashariki na kwamba mashabiki wamefurahia burudani Arusha na wataendelea kufurahia zaidi katika mikoa mingine. “Tutawaletea wasanii wenye hadhi kulingana na mapendekezo ya mashabiki husika wa mkoa huo, tena wale waliojizolea sifa ndani na nje ya nchi,” alisema. | 1 |
WASHINGTON, MAREKANI KAMATI za Bunge la Marekani zinazoendesha uchunguzi dhidi
ya Rais Donald Trump zimeiamuru Ikulu ya White House kuwasilisha nyaraka zote
za mawasiliano kati ya Trump na Ukraine. Amri hiyo imetolewa baada ya Ikulu ya Marekani kushindwa
kuchapisha kwa hiyari nyaraka hizo kabla ya kumalizika kwa muda wa mwisho juzi Ijumaa. Mmoja wa viongozi wa kamati za Bunge la Marekani amesema
ni wazi Rais Trump amechagua njia ya kuficha ukweli baada ya kushindwa kwa
mwezi mzima kuweka wazi nyaraka za mawasiliano yake na Ukraine. Juzi Rais Trump
alisema huenda asitoe ushirikiano kwenye uchunguzi dhidi yake ambao unahusu
madai kwamba alimshinikiza rais wa Ukraine kumchunguza makamu wa rais wa zamani
Joe Biden na mwanawe kwa tuhuma rushwa. Trump ambaye tayari anakabiliwa na shutuma hiyo inayoweza
kumwondoa madarakani, juzi aliibuka na kauli mpya akiitaka China nayo imchunguze mpinzani wake huyo, Biden Hayo yamejiri siku chache baada ya mazungumzo ya siri ya
simu ya Trump na Rais wa Ukraine yanayotajwa kuwa na nia ya kumsambaratisha
mpinzani wake kisiasa, Biden kunaswa, na Ofisa wa Shirika la Kijasusi la CIA. Mazungumzo ya simu kati ya rais Trump na kiongozi wa
Ukraine Rais Volodymyr Zelensky,Julai 25 yalisababisha wapelelezi kupeleka
taarifa zinazoweza kumuondoa Trump madarakani. Ingawa siku ya alhamisi, rais Trump alidai kuwa madai
hayo ni upuuzi. Katika ujumbe wake wa usiku wa manane kupitia kurasa yake
ya Tweeter, Trump aliongeza kuwa yeye ana jukumu la kuchunguza kashfa za
rushwa, jambo ambalo linajumuisha kuuliza na kutoa mapendekezo kwa nchi jirani
kutoa msaada. Trump anamshutumu Biden na mtoto wake Hunter kwa kashfa
za rushwa katika mikataba yao ya kibiashara na kisiasa nchini Ukraine na China, Wakati ambao Hunter Biden alipoingia katika mkataba wa
gesi asilia katika katika kampuni ya Burisma mwaka 2014, maswali mengi
yaliibuka kuwa anaweza kumletea mgogoro kisiasa baba yake. Ukraine ilikuwa inakabiliana na mgogoro wa kisiasa baada
ya kiongozi wake kulazimishwa kuondoka madarakani, wakati huo Biden alikuwa
Makamu wa Rais katika utawala wa Barack Obama. Mwaka 2016, Biden aliishinikiza Serikali ya Ukraine
kumfukuza mwendesha mashitaka Viktor Shokin, ambaye ofisi yake ilikuwa
inaichunguza kwa karibu mmiliki wa kampuni ya Burisma. Katika hotuba yake mwaka jana Biden alijisifia kwa
kumfukuza Shokin na kutishia kutotoa mkopo wa mamilioni ya fedha kwa Ukraine. Trump na washirika wake wanamshutumu Biden kwa kumlinda
mwanae. Kama maofisa wengine wa Serikali ya Ukraine pia walitaka
Shokin aondoke madarakani kwa sababu ya jitihada zake za kukabiliana na rushwa. Wiki iliyopita mwendesha mashtaka nchini Ukraine ambaye
alichukua wadhifa wa Shokin aliliambia Shirika la Utangazaji la Uingereza la
BBC kuwa hakuna ushaidi wa uovu alioufanya Joe au Hunter Biden. Trump alipohojiwa kuhusu mazungumzo yake ya simu na rais
wa Ukraine, Volodymyr Zelensky alijibu kuwa; jibu ni rahisi kuwa ; “Nilidhani kuwa wameanza kufanya uchunguzi tayari
kama kweli walikuwa na nia njema basi wangeanza kumchunguza Biden,” “Vilevile, China pia inapaswa kuanza kumchunguza
Biden kwa sababu kile kilichotokea China ni sawa na kile kilichotokea
Ukraine”, Trump aliongeza. Msemaji wa Biden wa kampeni za mwaka 2020 amemshutumu
Trump kwa kutumia vibaya televisheni ya taifa kwa kutoa taarifa za kusadikika. Naye msemaji wa Hunter Biden ameviambia vyombo vya habari
vya Marekani kuwa kiwango cha dola bilioni 1.5 ni hesabu ya uongo, hawajahi
kupokea fidia yoyote ya malipo ya kiwango hicho cha fedha katika kiwanda
chochote China. Mwaka 2013, Biden
alipokuwa makamu wa rais alipofanya ziara ya kikazi nchini China na kukutana na
rais wa nchi hiyo, Xi Jinping, Hunter Biden na binti yake waliongozana naye. Biden alikuwa makamu wa rais wa kwanza kuongozana na
familia yake katika shughuli za kikazi. Katika ziara hiyo ya siku mbili , Hunter alikutana
mfanyakazi wa benki wa nchini humo, Jonathan Li, ambaye baadae akawa mshirika
wake katika biashara. Li alipata ufadhili binafsi muda mfupi tu baada ya ziara
hiyo ingawa msemaji wa Hunter alikiambia chombo cha habari cha NBC News kuwa
hawakujadili masuala yoyote ya kibiashara katika ziara ile na ufadhili ulikuja
miezi michache baadae. Hunter amekanusha kuwa na mkutano wowote kuhusu biashara
na ofisa wa China. | 2 |
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla ameitaka Taasisi ya Utafi ti ya Wanyamapori (TAWIRI) kuwa na mkakati na mpango kazi kwa mnyama aina ya twiga katika hifadhi mbalimbali nchini, kwani kuna viashiria vya wanyama huyo kutoweka katika hifadhi hizo.Alisema hayo jana wakati akifungua kongamano la 12, lililoshirikisha nchi 16 la wanasayansi watafiti wa uhifadhi duniani, wakurugenzi na watendaji wa taasisi za uhifadhi wa ndani na nje na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.Dk Kigangwalla alisema katika mpango kazi huo wa miaka mitano wa utafiti wa wanyama, Tawiri wanapaswa kuweka mkazo wa kujua nini kinasababisha twiga kutoweka katika hifadhi za taifa na kuja na majibu ya msingi juu ya hali hiyo ili serikali itayafanyia kazi haraka iwezekanavyo.Alisema twiga ni nembo ya Taifa, hivyo ni wajibu wa wanasayansi watafiti wa Tawiri, kuhakikisha wanapata majibu ya msingi kuhakikisha mnyama huyo hatoweki, bali anaongeze katika mbuga za Taifa.Akizungumzia utafiti mwingine ambao Tawiri inapaswa kuufanyia kazi ni pamoja na aina ya ndege, wajulikanao kwa jina la ndege wa ukanda wa Magharibi mwa Tanzania. Alisema kuwa ndege hao ni kivutio kikubwa katika kuvutia watalii nchini.Alisema katika ukanda huo, kuna ndege aina ya 700 katika eneo hilo la Magharibi mwa Tanzania, hivyo taasisi hiyo inapaswa kufanyia kazi na kuyapeleka mapendekezo yake serikali ili kiwe kivutio kikubwa kwa watalii nchini.Aidha, aliagiza kuweka nguvu zaidi kati suala jingine la migogoro ya binadamu na wanyama na mito kwa mamba na kiboko ili kuwajengea uzio.Mkurugenzi Mkuu wa Tawiri, Dk Saimon Mduma alisema changamoto zote, zilizosemwa na waziri asilimia kubwa zimeshaanza kufanyiwa kazi na mapendekezo yake, yatafikishwa serikalini kwa utekelezaji. | 3 |
PATRICIA KIMELEMETA MSAJILI wa Vyama Vya Siasa, Jaji Fransic Mutungi amesema hana mamlaka ya kutoa vibali vya kufanyika kwa mikutano ya ndani au nje pamoja na maandamano kwa vyama vya siasa. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya watu mbalimbali kumlalamikia Jaji Mutungi kuwa amekuwa akinyamazia ukiukwaji wa sheria ya uanzishwaji wa vyama vya siasa ambayo inavipa uhuru wa kufanya mikutano kama moja ya kazi zake. Msajili huyo pia anatupiwa lawama kwamba anakibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuruhusu viongozi wake kuendelea kufanya mikutano ya ndani na nje, huku vyama vingine vikizuiwa kufanya mikutano. Miongoni mwa vyama vinavyozuiliwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambapo baadhi ya viongozi wake wamekamatwa katika maeneo mbalimbali na kuwekwa mahabusu kwa amri za wakuu wa wilaya. Akizungumza na MTANZANIA katika mahojiano maalum ofisini kwake Dar es Salaam jana, Jaji Mutungi alisema wenye mamlaka ya kutoa vibali vya mikutano ya vyama vya siasa ni Jeshi la Polisi kulingana na eneo husika na si ofisi yake. “Nimeshangazwa kusikia wanasiasa wananipa lawama ya kuwaruhusu CCM kufanya mikutano ya kisiasa huku vyama vingine nikivizuia ili visiweze kufanya mikutano, wakati wanajua kuwa sina mamlaka ya kutoa kibali cha mikutano, ” alisema. Jaji Mutungi alisema sheria ya vyama vya siasa inatoa mwongozo kuhusiana na suala hilo na kwamba kama kuna tatizo lolote wanapaswa kuandika barua ya malalamiko kwenda Baraza la Vyama Vya Siasa ili yaweze kushughulikiwa kisheria. “Wanasiasa wanajua sheria ya vyama vya siasa inasemaje, lakini wanashindwa kuifuata badala yake wanaanzisha lawama zisizo na msingi ili ofisi yangu ionekane inatuhumiwa. “Nipo hapa kwa ajili ya kuvisimamia vyama vyote vya siasa iwe CCM, Chadema, CUF, NCCR -Mageuzi, TLP na vyama vingine, hivyo malalamiko ya kukibeba chama kimoja hayapo na hayo ni maneno yao tu. “Hakuna sera, kanuni au katiba ambayo inatoa mwongozo kwa vyama vya siasa vinavyopata matatizo kukimbilia kwenye mitandao ya kijamii au vyombo vya habari ili kuwasilisha malalamiko yao, lakini wanasiasa wamekuwa wakiwatumia wanahabari badala ya kuandika barua kwa baraza la vyama vya siasa, jambo hilo siyo zuri,” alisema Jaji Mutungi. Katika hatua nyingine Msajili huyo alikataa kuzungumzia hatua ya Chama Cha CUF kuingia katika mgogoro na Chadema, akisema mgogoro huo upo mahakamani si vema yeye kuuzungumzia. Alisema vyama vingine kuingilia mgogoro huo ni sawa na kukiuka katiba ya nchi ambayo inamtaka kila mwananchi kuheshimu katiba na kama suala lipo mahakamani halipaswi kujadiliwa mpaka mahakama itakapotoa hukumu. “Nimeshindwa kuelewa Chadema na CUF wanaingiaje kwenye mgogoro wakati ni vyama viwili tofauti na tayari CUF wenyewe wamefungua kesi mahakamani wanasubili uamuzi,” alisema. | 3 |
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) yenye jukumu la kukadiria, kukusanya na kuhasibu mapato ya serikali, ni miongoni mwa taasisi za umma zilizo mstari wa mbele kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa vitendo katika kutekeleza azma ya serikali ya kuleta maendeleo.Serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha miaka mitatu, imefanikiwa kuongeza makusanyo ya mapato kutoka wastani wa Sh bilioni 850 kwa mwezi mwaka 2015 hadi kufikia wastani wa Sh trilioni 1.3 kwa mwezi kwa sasa. TRA imeendelea kuongeza ukusanyaji wa mapato. Mwaka 2015/16 makusanyo yalikuwa Sh trilioni 12.5, mwaka 2016/17 yaliongezeka hadi kufikia Sh trilioni 14.4 na mwaka 2017/18 yaliongezeka hadi Sh trilioni 15.5.Mapato yote yaliyokusanywa kwa miaka mitatu mfululizo ni Sh trilioni 42.4. Taarifa ya makusanyo ya robo ya kwanza ya mwaka huu wa fedha 2018/19 kuanzia Julai hadi Septemba 2018 inaonesha TRA imekusanya Sh trilioni 3.84 ikilinganishwa na Sh trilioni 3.65 zilizokusanywa katika kipindi kama hicho mwaka wa fedha wa 2017/18.Ongezeko hili la ukusanyaji mapato ni hatua kubwa nchini ambalo kwa kiwango kikubwa limechangiwa na kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi na umma kumwelewa Rais hivyo kujitoa kwa dhati kumuunga mkono.Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa pamoja na viongozi wengine wa serikali wamekuwa wakishiriki mapambano dhidi ya ukwepaji kodi unaosababisha upotevu wa mapato ya nchi. Juhudi za Rais Magufuli zimeshuhudiwa akitekeleza kwa vitendo ahadi mbalimbali alizotoa ikiwamo ya wakati akifungua rasmi bunge la 11 mkoani Dodoma; Novemba 20, 2015. Aliahidi kupambana vikali na ukwepaji kodi na upotevu wa mapato ya serikali.Akifungua Bunge hilo, Rais Magufuli aliahidi kupambana na ukwepaji kodi na upotevu wa mapato ya serikali. Katika kipindi cha uongozi, ameongoza na kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari pamoja na kukemea udanganyifu unaofanyika kwenye risiti za kielektroniki (EFDs). Wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Morogoro mpaka Makutupora jijini Dodoma, Rais alisisitiza kuwa kodi husaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini na kuboresha huduma za jamii.“Napenda kuwahimiza Watanzania wote kuendelea kulipa kodi ili kutekeleza miradi ya maendeleo nchini pamoja na kuboresha huduma mbalimbali za kijamii. Pamekuwepo na mtindo, mtu anapokwenda kununua bidhaa anapewa risiti ya bei ndogo badala ya risiti anayotakiwa kupewa.” “Mtoa risiti na mpokeaji wote kwa pamoja wanaiibia serikali na hivyo wanasababisha kuchelewesha maendeleo, ninawaomba Watanzania tuwe wazalendo,” alisema.Licha ya ongezeko la makusanyo, ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Magufuli, TRA imeboresha mifumo yake ya ukusanyaji mapato kumrahisishia mwananchi kulipa kodi stahiki na kwa wakati. Miongoni mwa hatua zilizofanyika ni a uhakiki wa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) kuboresha daftari la walipakodi na kuifanya itumike katika kufanya mawasiliano na TRA hususani katika huduma za kielektroniki.Katika muktadha wa kuhakikisha watu hawakwepi kulipa kodi, TRA imeendelea kudhibiti uingizaji wa bidhaa za magendo nchini kwa kuimarisha doria sehemu za mipakani na mipaka isiyo rasmi ambayo ni maarufu kwa kupitisha bidhaa za magendo. Udhibiti huu unalenga kuhakikisha bidhaa zote zinazoingizwa nchini zinapitia njia rasmi na zinalipiwa kodi na ushuru stahiki kwa mujibu wa sheria, ikiwa pia ni njia mojawapo ya kulinda viwanda vya ndani.Aidha, TRA kupitia Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi imejikita kuhudumia na kuelimisha walipakodi na wadau mbalimbali waelewe umuhimu wa kulipa kodi kwa hiari kwa manufaa yao na taifa kwa jumla. Kupitia idara hiyo, mamlaka imefanikiwa kuongeza uelewa wa masuala ya kodi kwa wananchi. Hivi sasa semina, vyombo vya habari, machapisho, makongamano, tovuti, mitandao ya kijamii pamoja na kituo cha huduma kwa mteja kilichopo ndani ya TRA hutumika zaidi kufikisha ujumbe kwa walipakodi.Mafanikio mengine ni ufunguzi wa vituo vya pamoja vya huduma mipakani. Miongoni mwa vituo hivyo ni kituo cha Rusumo kilichopo mkoani Kagera kilichozinduliwa Aprili, 2016 na Rais Magufuli pamoja na Rais wa Rwanda, Paul Kagame. Kituo kingine ni cha Mtukula kilichopo mkoani Kagera kilichozinduliwa na Rais John Magufuli na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni Novemba, 2017.Vituo vingine ni Holili kilichopo mkoani Kilimanjaro na Tunduma cha mkoani Songwe. Vituo hivi kwa pamoja husaidia kuharakisha utoaji wa huduma mipakani, kuokoa muda wa kushughulikia mizigo na abiria, kukuza biashara na hatimaye kuongeza ukusanyaji wa mapato baina ya nchi zinazopakana. Sambamba na hayo, serikali imeendelea kuwajali na kuimarisha uhusiano na wafanyabiashara nchini. Kwa kipindi cha miezi sita kuanzia Julai mosi hadi 31 Desemba mwaka huu, serikali TRA imetoa msamaha maalumu wa riba na adhabu katika malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia 100 na mwisho wa kuwasilisha maombi ya msamaha huo ni Novemba 30, 2018.Msamaha huo unalenga kutoa unafuu kwa walipakodi wenye mzigo wa malimbikizo ya madeni ya kodi kwa kuwapa fursa ya kulipa kodi ya msingi (principal tax) baada ya kuondoa riba na adhabu kabla ya Juni 30, 2019. Hadi mwishoni mwa Oktoba mwaka huu, TRA ilipokea maombi ya kusamehe riba na adhabu kutoka kwa walipakodi 2,029 yanayofikia Sh bilioni 245.6.Baadhi ya walipakodi hao wameshapewa majibu na wengine wako katika hatua mbalimbali za kushughulikiwa maombi yao. Kuondoa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi ni hatua mojawapo ya kusaidia wafanyabiashara wenye malimbikizo hayo kutokukwepa kulipa kodi, ikiwa ni sehemu ya ahadi ya Rais Magufuli ya kuhakikisha kuwa, mianya ya ukwepaji kodi inadhibitiwa ipasavyo. Pamoja na mafanikio yote haya, TRA imedhamiria kuongeza kasi ya usajili wa walipakodi wapya, kuendelea kutoa huduma na elimu kwa walipakodi, kuendelea kudhibiti biashara za magendo pamoja na wakwepakodi kuhakikisha kuwa kunakuwa na ongezeko la ukusanyaji wa mapato yatakayoiwezesha nchi yetu kufikia uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo mwaka 2025. | 3 |
Timu hiyo ilitembelea kituo hicho ikiwa na wachezaji wake 25 na viongozi wake baada ya kuwasili mkoani kwa ajili ya kucheza mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Kambarage.Akizungumza mbele ya watoto hao msemaji wa Simba, Haji Manara ambaye alishindwa kujizuia huku akibubujikwa na machozi alisema kuwa klabu hiyo imekuwa ya kwanza nchini kutembelea kituo hicho na kutoa msaada na sababu ya kufanya hivyo ni kuona changamato ya mauaji ya albino Kanda ya Ziwa imekuwa kubwa.“Msijione wanyonge, msikate tamaa ya maisha na kujitenga na jamii kwa kuwa ni albino, mbona mimi ni albino na nimepitia nafasi mbalimbali za uongozi hivyo nanyi msome mfanye bidii nipo nyuma yenu nitahakikisha nawaleta wafadhili katika kituo hiki ili muweze kusaidiwa,” alisema Manara.Naye Ibrahimu Twaha aliyesoma risala katika kituo hicho kwa niaba ya wachezaji wenzake alishindwa kusoma risala hiyo kikamilifu baada ya kutoa maneno ya awali yenye uchungu na kuishia kutokwa na machozi.“Ninyi ni ndugu zetu Mungu ni mmoja wanaofanya kitendo cha kuwaua au kuwadhuru albino wanatenda dhambi hata Mungu hapendi katika dini zote,” alisema Twaha. | 4 |
Msanii na boss wa lebo ya pozi kwa pozi (PKP), Ommy Dimpoz amesema, hajaumizwa na msanii mwenzake TID licha ya msanii huyo kumtaja yeye katika list ya wasanii watano wabovu Tanzania. TID alipost listi hiyo kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter huku akiwaweka wasanii Benpol, Dimpoz, Abdu Kiba na Mwasiti kama wasanii wabovu bongofleva. Akiongea katika mahojiano na EATV Dimpoz amesema hana uhakika kama ni TID amefanya hivo sababu yeye hayupo Twitter sababu akaunti yake imehakiwa. Amesema, licha ya hivyo nchi hii ni huru na kila mtu ana mtazamo wake na uhuru wa kuongea anavyojiskia. “Kila mtu ana maoni yake na TID ni braza wetu, mwisho wa siku tuko katika nchi huru. kwangu mimi ukiniuliza kuhusu TID ntakuambia ni msanii bora kati ya wasanii bora waliowahi kutokea,” alisema Dimpoz. Kuhusu ziara ya kimuziki ya rafiki yake Ally Kiba amesema amejipanga vyema ili kuendana na ziara hiyo iitwayo AliKiba Unforgettable Tour. Ommy Dimpoz ameeleza kuwa ziara hiyo ni ya kifamilia hivyo ni lazima awepo. “Unajua hii ni ‘Tour’ ya kifamilia, naweza kusema hivyo, pia Ali Kiba ni mtu wangu, kwahiyo kuna tarehe ambazo nitakuwepo kweli kwenye show, naweza kusema nimejipanga pia nina msisimuko, nipo tayari kutoa msaada kwa ndugu yangu na nimejipanga” amesema Ommy Dimpoz. Ziara hiyo ya kimuziki ya Ali Kiba, tayari imeshaanza mkoani Tabora, tangu walipowasili siku ya Jumatano ya Novemba 27, 2019, ambapo watakuwa pamoja na timu nzima ya East Africa Radio na East Africa Television. Ndani ya ziara hiyo Ali Kiba atafanya shughuli za kijamii, kutembelea vyuoni, kutoa misaada kwa wagonjwa, kucheza mpira pamoja na show yenyewe itakayofanyika siku ya Jumamosi ya Novemba 30, katika viwanja vya Ali Hassan Mwinyi kuanzia saa 12 jioni. | 1 |
THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM KIKOSI cha Simba chini ya Kocha Mkuu, Patrick
Aussems, kimeendelea kujifua kwa mazoezi sambamba na mbinu tofauti kwa ajili ya
kuhakikisha kinaitupa nje ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, timu ya UD
Songo ya Msumbuji. Wekundu hao watakuwa wenyeji wa UD Songo, katika
mchezo wa marudiano wa hatua ya awali ya ligi hiyo utakaochezwa Jumapili hii
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mchezo wa kwanza ulichezwa jijini Beira nchini
Msumbuji, ambapo Simba ililazimisha suluhu. Matokeo hayo yanaufanya mchezo wa marudiano kuwa
mgumu zaidi kwakua kila upande una fursa ya kusonga mbele, ikiwa utapata
ushindi. Jana asubuhi kikosi cha Simba kiliendelea na
mazoezi kwenye Viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam, ambapo MTANZANIA
lilishuhudia Aussems akitumia muda mwingi kwenye zoezi la kupiga mashuti nje ya
18. Pia alionekana akiwapika viungo wake Sharaf Eldin
Shiboub, Jonas Mkude, Fransic Kahata, Hassan Dilunga na Mzamiru Yassin, ili
kama safu yake ya ushambuliaji inayoongozwa na Meddie Kagere itabanwa wao
watumie mwanya huo kufunga. Akizungumza baada ya mazoezi yao, Aussems alisema
wataingia uwanjani na pango tofauti na ule wa Beira, kwani safari hii
watashambulia zaidi ili kusaka mabao na hatimaye waweze kuibuka na ushindi. “Ugenini tulilenga zaidi kuhakikisha haturuhusu
bao na tulifanikiwa, tutakuwa na mpango tofauti kwenye mchezo wa marudiano
ambao ni kushambulia zaidi kwakua tunahitaji ushindi na si kingine,”
alisema raia huyo wa Ubelgiji. | 4 |
Kocha Mkuu wa Tanzania Emmanuel Amunike amesema michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika imekuwa ni funzo kubwa kwa Taifa Stars baada ya kutolewa mapema nchini Misri. Tanzania, ambao imerejea kwa mara ya kwanza kwenye michuano hiyo baada ya miaka 39, imeshindwa kusonga mbele katika hatua ya mtoano baada kumaliza mkiani mwa kundi lao kwa kukubali kichapo kwenye mechi zote tatu walizocheza. Kwa winga huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria na klabu ya Barcelona, hilo lilikuwa funzo kubwa ya kuwa ni namna gani mpira barani Afrika umebadilika na kuimarika.
“Ni somo kubwa kwa mpira wa Tanzania. Hatukuwahi kushiriki toka mwaka 1980, mambo mengi yametokea ndani ya miaka 39, na mpira umebadilika na unaendelea kubadilika,” Amunike amesema. “Kitu cha msingi ni kuendana na mabadiliko haya na kuimarika kama timu. Kuna mengi ya kujifunza. “Shida yetu kubwa ilikuwa ni kutokuwa na uzoefu. Hatuna uzoefu wa kutosha sababu tumezoea kucheza mpira bila kuwa na shinikizo kubwa.” “Lakini tumeona katika michuano hii pale unapokuwa na mpira, basi wapinzania wanakuweka katika shinikizo kubwa.” Tanzania ilionesha dalili njema kwenye mchezo wao dhidi ya majirani Kenya, lakini ilishindwa kabisa kufurukuta dhidi ya Senegal na Algeria. Amunike, ambaye alinyanyua Kombe la Dunia 2015 akiwa kocha wa timu ya vijana wa chini ya miaka 17 Nigeria, amesema Tanzania itabeba mafunzo yote waliyoyapata baada ya kurejea kwenye ulimwengo wa kandanda la ushindani. “Hatukuwa wenye kujiamini ama kutulia pale ambapo tulikuwa tunamiliki mpira.” “Katika kila safari, kuna mchakato wa kujifunza. Tutakaporejea (nyumbani) itatupasa tujitathmini kwa undani na kuona ni kwa namna gani tutaboresha mpira wetu. “Ni dhahiri kuwa katika mpira wa kisasa, kama huna uwezo wa kushindana hutakuwa na nafasi ya kushinda – na hilo ndilo tulilokutana nalo.” Amunike ambaye alishinda taji la Mchezaji Bora wa Afrika mwaka 1994 pia anaamini kuwa kuna mustakabali mzuri kwa soka la Tanzania. “Ninafurahishwa na wachezaji wangu, wote tulifanya kazi kubwa mpaka kufikia hapa, hatukualikwa tulishinda,” amesisitiza. “Kama tutaendelea na ari hii, na kuboresha katika yale tufanyayo naamini tutakuwa kama timu.” Maoni ya wadau | 4 |
Na ASHA BANI-DAR ES SALAAM BAADHI ya wenyeviti wa Serikali za mitaa wa Chama cha Wananchi (CUF), Mkoa wa Dar es Salaam, wamemuunga mkono Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad huku wakigomea uamuzi wa kuitwa kuhojiwa na Mwenyekiti anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba. Kutokana na hali hiyo wamesema kuwa kiongozi huyo hana sifa ya kufanyakazi wala kuwahoji kwani alishapoteza sifa ya kukiongoza chama hicho kwa mujibu wa katiba ya CUF. Licha ya hali hiyo viongozi hao pia wameunga mkono tamko la Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani, Saed Kubenea la kushirikiana katika operesheni yao inayojulikana kwa jina la ‘Ondoa Msaliti Buguruni’(OMB) iliyotangazwa kuanza hivi karibuni. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kwa niaba ya wenyeviti hao, Mwenyekiti wa Mtaa wa Mtambani Manispaa ya Kinondoni, Bakari Kasubi alisema Profesa Lipumba hana sifa ya kuwaita kwani alishafukuzwa uanachama ndani ya chama hicho. “Tunasikia eti wanaojiita viongozi wa chama walipora mamlaka isiyo yao wanaandaa utaratibu wa kuwaita baadhi ya wawakilishi wa chama, madiwani, wabunge na viongozi wa serikali za mitaa kwa kile kinachoitwa kwenda kuhojiwa na kamati ‘feki’ ya maadili ya chama, hatuwezi kuhojiwa na watu hao,’’ alisema Kasubi. Alisema wao wenyeviti wanaunga mkono juhudi na mwelekeo uliochukuliwa na chama chao kutokana na maamuzi ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa na msimamo wa chama uliotolewa na Katibu Mkuu wao Maalim Seif Sharif Hamad. Alisema wenyeviti wanaungana kupinga maamuzi ya RITA mbele ya Mahakama Kuu kwa kufungua kesi ambayo kwa mujibu wa kifungu cha 26 kwa kukiuka taratibu za sheria ya wadhamini na kesi nyingine zinazohusiana na hujuma ambazo walitaja kuwa ni fedha za ruzuku. “Tunapingana kwa nguvu zote njama na mipango ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi kwa kushindwa kuheshimu hadhi na nafasi yake mbele ya jamii na kujiingiza katika vitendo vya hovyo vyenye muelekeo wa kutaka kuiharibia mustakabali wa CUF na kuwaathiri wadau mbalimbali walioshiriki katika kuasisi na kuijenga kwa takribani miongo miwili na nusu sasa,’’alisema Kasubi. Alisema wanampinga Profesa Lipumba kwa kukubali kutumiwa na CCM kwa masilahi yao binafsi na kushindwa kuthamini mchango wa CUF katika kujenga demokrasia nchini. “Lipumba leo amekuwa mtu wa kuweweseka ameshindwa kutumia taaluma yake kwa masilahi ya taifa, kila kukicha anatafuta msaada kwa vyombo vya dola ili kufanikisha dhamira yake, ameshindwa kukemea vitendo viovu vinavyoendelea kufanywa na wafuasi wake wanapohudhuria mahakamani, kushambulia waandishi wa habari kauli za kashfa na kejeli dhidi ya viongozi ,’’alisema . Aliongeza kuwa wito wao kwa wanachama na viongozi wa CUF kujiandaa vyema kukabiliana na mfumo kandamizi wa demokrasia nchini na kuwashughulikia wale waliowaita vibaraka wanaotumika katika kuharibu demokarsia na kukivuruga chama hicho. | 3 |
NA AZIZA MASOUD, KILA mtoto anazaliwa na kipaji chake, yupo anayezaliwa na kipaji cha kuimba, kucheza mpira na ubunifu wa vitu mbalimbali, tatizo kubwa ni katika kuviendeleza. Kwa maana hiyo, watoto wanazaliwa wakiwa na vipaji ambavyo vikiendelezwa huwasaidia katika maisha yao ya kila siku. Nimeona mara kadhaa wazazi/walezi wakiwakataza watoto wao kufanya baadhi ya vitu kwa madai kuwa havina faida kwenye maisha yao, wapo ambao hawapendi kuona watoto wao wakicheza mpira, kwani huona kuwa wanapoteza muda na mchezo huo hauna maendeleo kwenye maisha yao. Nimeshuhudia pia mzazi akimkataza mtoto wake wa kike kuimba kwa madai kuwa, jambo hilo halina faida kwa maisha yake ya baadaye. Ni kweli kwa mzazi ambaye anapenda maisha mazuri ya mtoto wake na anayeamini katika ajira za kuajiriwa hatapenda kuona mtoto wake anacheza mpira au kuimba, wengi wanaamini mambo hayo yanapoteza muda kwasababu hajayaandaliwa mazingira mazuri. Lakini ni vyema wazazi wakaelewa kuwa, kumsaidia mtoto kuendeleza kipaji chake kunaweza kuwa na maana kubwa katika maisha yake ya baadaye, karne hii ya sasa watu ambao wamejiajiri kupitia vipaji vyao wengi wamefanikiwa, kikubwa kinachotakiwa ni kuwa mstari wa mbele kumsaidia kutambua mbinu anazotakiwa kuzifanya kwa ajili ya kufanya mambo yenye faida. Anza hivi Kwanza gundua kipaji, chunguza na uone anafanya mambo gani ambayo unaweza kumsaidia kuyaendeleza. Mweleze faida zake na hasara zake, msaidie kujiendeleza, huku ukihakikisha anafanya vizuri kwenye masomo yake, kwani ndiyo yatamuweka kwenye nafasi nzuri ya kuendeleza kipaji chake. Mweleze muda muafaka wa kufanya mambo yake, mtengenezee misingi mizuri, kwa maana kwamba hata akiingia huko kwenye kujiendeleza asije akatetereka. Muonye kutojihusisha na mambo mabaya, kama ana kipaji cha uimbaji mueleze madhara ambayo anaweza kupata kama hataingia kwa malengo maalumu, jaribu kumueleza kwamba, yeye awe kama yeye na si kufuata mkumbo. | 0 |
NAHODHA wa timu ya Soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Mbwana Samatta leo anatarajia kuichezea kwa mara ya kwanza Aston Villa tangu akuposajiliwa kutoka Genk ya Ubelgi.Aston Villa inashuka dimbani kumenyana na Leicester City katika mchezo wa nusu fainali ya pili ya Kombe la Carabao utakaofanyika kwenye Uwanja wa Villa Park, huku Samatta akitegewa katika safu ya ushambuliaji.Samatta alisajili wa Aston Villa hivi karibuni huku akitegemewa sana na timu hiyo ambayo ilikuwa haifanyi vizuri katika Ligi Kuu ya England.Tayari kocha wa timu hiyo, Dean Smith amethibitisha kutaka kumpanga Samatta huku akiwa na matumaini makubwa na mshambuliaji huyo baada ya safu ya ushambuliaji ya Aston Villa kuwa na matatizo baada ya kukumbwa na majeruhi na wengine kuondoka katika timu hiyo.Hata hivyo, nahodha huyo wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, anatarajia kukumbana na upinzani mkali kutoka kwa beki kisiki Mturuki Caglar Soyuncu.Aidha, mchezo huo ambao unatarajiwa kutazamwa na mamilioni ya Watanzani wengi baada ya Samatta kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza katika klabu ya Ligi Kuu ya England.Licha ya Villa kupewa nafasi ya kuibuka na ushindi kwa faida ya uwanja wa nyumbani, bado mchezo huo wa marudiano unatarajiwa kuwa mgumu kwa pande zote kutokana na matokeo ya mechi ya awali, ambayo walitoka sare ya 1-1, na ubora wa Leicester kwa sasa.Kocha Smith aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Samatta amekuwa na mwenendo mzuri mazoezi tangu ajiunge na klabu hiyo, hivyo kuna nafasi kubwa ya kumchezesha katika mchezo huo wa leo. | 4 |
Na CLARA MATIMO, MWANZA SHULE za msingi 15 za Serikali zilizopo Halmashauri ya Jiji la Mwanza, zimepatiwa msaada wa vifaa mbalimbali vya sekta ya elimu vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 50 kutoka shirika la Brac Maendeleao Tanzania, tawi la Mwanza. Shirika hilo, limetoa msaada huo ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa kuwasaidia watoto wa kike wanaokumbwa na changamoto, wakati wa masomo ‘Girls Education Challenge (GEC) ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2014 katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Singida, Tabora na Dar es Salaam. Shule zilizopatiwa msaada huo, ni Iseni, Amani, Nyabulogoya, Pamba B na C, Mabatini A na C, Bugarika, Miembeni, Nyakabungo, Lake, Nyashana, Nyakurunduma, Tambuka Reli na Mbungani. Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo mwishoni mwa wiki iliyopita kwa Mbunge wa Nyamagana, Stanslaus Mabula, Meneja Mradi wa GEC, Kanda ya Ziwa, Shahinoor Rahman, alisema lengo la mradi huo ni kuwasaidia watoto wa kike waliokata tamaa ya kuendelea na masomo kutokana na changamoto mbalimbali. | 3 |
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad (pichani) ameonesha ushirikiano mkubwa wakati wa kuhojiwa na Kamati ya Kudumu ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.Akizungumza na vyombo vya habari jijini hapa jana baada ya kufanya mahojiano na CAG kwa saa 3.40, Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Emmanuel Mwakasaka alisema kiongozi huyo alionesha ushirikiano mkubwa katika muda wote wa mahojiano.“CAG ameitikia mwito uliomtaka kufika hapa na ameonesha ushirikiano mkubwa katika kujibu maswali tuliyomuuliza.“Kamati inaendelea na shauri hili, tukikamilisha tunalipeleke kwa Spika wa Bunge kwa hatua nyingine,” ameAnnbXsema Mwakasaka.Alisema baada ya kufanya mahojiano hayo na CAG tangu saa 5.10 asubuhi hadi 8.50 adhuhuri, watachambua na kuandika ripoti na kuipeleka kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai kwa hatua zaidi.Kuhusu vielelezo alivyokuwa navyo CAG, Mwakasaka alisema ni kawaida kwa mtu akiitwa mbele ya Kamati anatakiwa kwenda na vielelezo vyake, hivyo navyo vitafanyiwa na kuingizwa kwenye ripoti hiyo atakayopelekewa Spika.Jana asubuhi, CAG aliitikia mwito wa Spika Ndugai alioutoa Januari 7, mwaka huu mbele ya vyombo vya habari wa kumtaka afike mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kuhojiwa kufuatia kauli yake kuwa, ‘Bunge ni dhaifu.’Profesa Assad aliwasili katika viwanja vya Bunge saa 4:47 asubuhi akiwa katika gari jeupe si lile, lililoandikwa CAG na kupitia katika geti, ambalo linatumiwa na wafanyakazi na Waziri Mkuu, ambapo alikaguliwa katika mashine kama watu wengine wa kawaida.Mara baada ya kuingia getini akiwa amebeba mabegi mawili madogo, alipokelewa na askari kanzu wa Bunge, ambaye aliambatana naye hadi kwenye lango la kuingilia jengo la utawala.Kabla ya kuingia jengo hilo, kama ilivyo desturi, pia alikaguliwa katika mashine na baadaye akaelekezwa mahali pa kuketi katika viti vya mapokezi, akisubiri kupewa maelekezo.Baada ya kuketi alifika na kusalimiana na Katibu wa Spika wa Bunge, Saidi Yakubu ambapo alipatiwa kitabu cha kusaini wageni na baada ya kusaini aliendelea kuketi akisubiri kuitwa kuingia ukumbini.Profesa Assad alitumia muda huo wa takribani dakika 10 hivi kufungua begi lake na kutoa nyaraka mbalimbali akaendelea kuzisoma. CAG aliitwa katika ukumbi wa Spika na kuingia ukumbini saa 5.05 asubuhi na dakika moja baadaye alikuwa tayari amekaa kwenye kiti cha wageni.Akiwa mbele ya wajumbe wa 17 wa kamati hiyo ,wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mwakasaka, aliwasha kompyuta mpakato baada ya kusalimia wajumbe wa kamati hiyo. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mwakasaka alimkaribisha Profesa Assad na kuwaomba waandishi wa habari watoke nje ya ukumbi, kwa kuwa kazi yao ya kupiga picha na kumshuhudia shahidi, ilikuwa imekamilika.Kwa mujibu wa kanuni za Bunge, baada ya kuhojiwa na Kamati hiyo, taarifa ya mahojiano itapelekwa kwa Spika wa Bunge na yeye atakuwa na uamuzi wa kuitisha mikutano na waandishi wa habari au kuliarifu Bunge. Sakata la Profesa Assad na Spika lilianza Desemba mwaka jana, wakati CAG alipohojiwa na Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa (UN) na akatamka kwamba Bunge ni dhaifu kutokana na kutofanyia kazi hoja ufisadi zinazopelekwa Bungeni na ofisi yake.Ndugai Januari 7, mwaka huu, alifanya mkutano na waandishi wa habari akimtaka CAG kufika mbele ya kamati hiyo kueleza kuhusu kauli yake aliyoitoa wakati anazungumza na Mwandishi huyo. Spika Ndugai alimkata CAG afike Januari 21,mwaka huu, kitendo ambacho ameitikia mwito huo.Hii ni mara ya kwanza kwa Spika kumwita CAG mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kitendo hicho kinalifanya Bunge la 11 kuandika historia nyingine, baada ya kuwaita viongozi wengine wa juu akiwemo Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti.Mwakasaka alisema, Kamati inaendelea na kazi yake leo ambapo Mbunge wa Kawe, Halima Mdee atafika mbele ya Kamati hiyo kujibu tuhuma za kuunga mkono kauli ya CAG kuwa Bunge ni dhaifu. | 3 |
KAMPUNI ya Simu ya Halotel itafi kisha mawasiliano katika vijiji 328, hatua ambayo pamoja na faida zingine itatoa fursa kwa wananchi wa maeneo hayo kunufahika na huduma mbalimbali inazotolewa na kampuni hiyo.Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Nguyen Van Son alipokuwa akizungumzia mafanikio yaliyofikiwa na kampuni hiyo katika kipindi cha mwaka jana na mipango mbalimbali kwa ajili ya mwaka huu. Alisema katika utekelezaji wa mpango huo unaofanywa na Halotel kwa ushirikiano na serikali kupitia mfuko wa Fursa Sawa kwa Mawasiliano kwa wote (UCSAF), jumla ya Sh bilioni tisa zimetengwa ili kufikia malengo hayo.Alisema utekelezaji huo ambao ni wa awamu ya tatu unaotarajiwa kufanywa hadi mwishoni mwa mwaka huu chini ya ushirikiano na UCSAF, umelenga kuwaondolea adha ya huduma za mawasiliano wananachi waliopo katika maeneo hayo, suala ambalo Halotel imekuwa ikilisimamia kwa umakini mkubwa. Alisema kupitia ushirikiao na UCSAF awamu ya pili ya utekelezaji, Halotel iliweza kufikisha mawasiliano katika vijiji 240 katika maeneo mbalimbali nchini.Aidha alisema Mwaka 2018 ulikuwa mwaka mzuri kwa Kampuni hiyo baada ya kufanikiwa kuongeza idadi ya wateja na mawasiliano katika maeno mbalimbali nchini. “Takwimu zilizopo zinaonyesha watumiaji wa mtandao wa Halotel hadi Septemba imeweza kufikia wateja milioni nne ilikua kutoka wateja milioni 3.7, Septemba Mwaka 2017. …Kadhalika, idadi ya watumiaji wa Halopesa ikiongezeka kwa kasi kutoka watumiaji 358,217 Septemba Mwaka 2017 hadi watumiaji 800,000 Setemba mwaka 2018,” alisema.Alisema katika kipindi hicho Halotel pia imeweza kuunganisha Optic Fiber zenye urefu wa kilomita 2,000 katika maeneo yenye miundombinu yake kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa data kwa maeneo mapya; kupitia hilo Halotel imeendelea kuwa chaguo la kwanza kwa wateja pale linapokuja suala la huduma za intaneti. “Hii ndio sababu tumeweza kuongeza dakika zaidi za kupiga kwenda katika mitandao yote hasa kupitia kifurushi cha kila kikimpta mteja unafuu wa hadi asilimia 32, lengo ni kumpa mteja kitu anachostahili kupitia offer hiii maalumu ni hii ilitokana na mahitaji hasa kwa wateja wa Dar es Salaam na Manyara,” alisema. | 3 |
KUNA watu wamepata umaarufu katika namna ya kuchekesha kidogo. Unamkumbuka yule aliyejiita Mganga wa Diamond? Katika namna isiyotarajiwa, eti ghafla na yeye akawa maarufu tena maarufu sana. Kila eneo akasifika. Kuanzia kwenye blog, magazeti hata katika baadhi ya vipindi vya televisheni akawa anatajwa kila wakati. Ila sasa yuko wapi? Yale maneno na ahadi alizotoa juu ya Diamond ziko wapi? Diamond bado anashikilia usukani wa Bongo Fleva huku yeye akiwa taabani.
Kama wengine na yeye pia alikuwa katika mbio za kusaka umaarufu na jina bila kutoa jasho. Nahisi alifanikiwa.
Siyo huko tu. Hayo yapo katika siasa, muziki hata filamu. Si yupo yule mwanasiasa aliyesema kama akichaguliwa bangi na mirungi itaruhusiwa? Na yupo yule mwingine badala ya kuuza sera zake, akaanza kujitapa kuwa anakaa Masaki na yeye ni mmoja kati ya watu matajiri Tanzania. Wa aina hiyo wapo.
Kila eneo wapo. Wengine baada ya kuona kila eneo limejaa wamejipachika umeneja na uongozi maeneo fulani. Si unamjua Ostaz Juma na Musoma.
Leo nimemkumbuka sana. Si unakumbuka kama alikuwa ni bosi fulani, pedeshee fulani na pia akajifanya mwanamuziki fulani?
Sitaki kuzungumzia alichowahi kukifanya kwa PNC. Ila angalia utendaji wake wa kazi kama meneja wa wasanii. Tangu alipowahi kuwachukua wakina Dogo Janja, Suma Mnazaleti, Amazoni na wengineo, kipi kikubwa alikifanya katika kuendeleza uwezo na vipaji vya wasanii hao?
Hata kwa jicho la kinyonga, unaweza kumfananisha Ostazi Juma na Musoma na Said Fella? Muangalie Aslay. Hukumu kipaji chake, kisha muangalie Dogo Janja wa kipindi cha Ostaz Juma pia hukumu kipaji chake. Wote hawa wawili wana vipaji vikubwa sana. Ila mmoja alikuwa kwa mtu makini na mwingine alikuwa na mtu mzushi ndiyo maana maendeleo yake kimuziki yalidumaa mpaka aliporudi tena kwa wanaojua kazi zao.
Kumiliki visenti kadhaa siyo tiketi ya kuwa meneja wa watu. Wenye uwezo na kazi hiyo wapo. Wakina Babu Tale wapo, wakina Alex Msama wapo. Hizi sifa na kutaka kuonekana fulani ana pesa zisishabikiwe sana hata kufanya vijana wenye vipaji ambavyo kimsingi ndiyo mkombozi wa maisha yao viishie kupotea.
PNC sio msanii mdogo. Tangu kitambo anafanya vizuri na ana ‘fan base’ kubwa tu. Ila kuna tatizo katika ukuaji wake wa muziki. Mbali na yeye mwenyewe kukosea katika mambo fulani, ila pia hata uongozi wake chini ya Ostazi Juma na Musoma ulimpotezea kabisa dira.
Zaidi ya kumsaidia hela mbuzi, Ostazi Juma kamsaidia kipi cha maana PNC? Au kumdhalilisha baada ya PNC kuhitaji msaada na kuweka hadharani ile video na jamii yote ijue ana matatizo, ndiyo msaada kwa anavyoamini?
Wakina Chief Kiumbe wana hela. Ila hata siku moja hatujawahi kuwasikia wakiwadhalilisha wakina Matonya au Tunda. Tofauti ipo. Kati ya uongozi bora na uongozi magumashi, tofauti ipo.
Dhima halisi ya meneja ni kumfanya muhusika akue kisanaa na sanaa iweze kumletea mafanikio halisi. Sio kumpa pesa mbuzi kisha kumdhalilisha.
Kwa watu aina ya Ostazi Juma, hata wangekuwa na wasanii aina ya Diamond, Barnaba na Ali Kiba, bado wasanii hao wasingeweza kufanya vizuri. Kwani tatizo haliko kwa wahusika wenyewe bali tatizo liko kwao kama mameneja.
Jaribu kumtafakari Dogo Janja wa Tip Top, kisha mtafakari alipokuwa Mtanashati. Wanafanana? Labda wa Tip Top hakuwa amewahi kwenda Afrika Kusini wala kutoka Arusha kwa ndege ila wa Mtanashati alienda. Ila ni nani alikuwa akitambulika zaidi kimuziki? Ni nani alikuwa akionekana kuwa ni nyota hatari ya baadaye? Kati ya Babu Tale na Ostazi Juma, tofauti ipo.
Suala sio fedha, ila ni namna gani unatumia vizuri fedha na akili yako kumfanya fulani aweze kufikia malengo yake. Katika hili Ostazi Juma alishindwa vibaya sana. ni kheri alivyowaachia wakina Fella wafanye kazi yao.
Eti katika hali kabisa ya ubinadamu na kujali, unaweza vipi kumdhalilisha mtu kama alivyomfanyia PNC kisha kusema kuwa wanastahili kufanyiwa hivyo? Hawa watu ni virusi katika sanaa yetu.
Hivi kama angekuwa anawaazima wasanii magari na kuwapangishia majumba kama anavyofanya Chief Kiumbe, ingekuwaje? Nina hofu siku moja angemtoa nje mtu usiku.
Haikuwa ujanja alichofanya Ostaz Juma kwa PNC. Kwa watoto wa mjini, waliokulia mitaa fulani ya mjini na kucheza hapa hapa town, kwao kitendo kile wanakiita cha kishamba huku waerevu wanakisema kuwa ni cha kilimbukeni. Leo nilimkumbuka sana huyu Meneja Magumashi
| 1 |
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Rosalynn Mworia
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC, imetangaza kuongeza muda wa uuzaji wa hisa zake hadi Mei 11.
Akizungumza Dar es Salaam jana Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Rosalynn Mworia, alisema hatua hiyo inatokana na kupokea maombi mengi ya kutaka kununua hisa za kampuni hiyo.
“Vodacom Tanzania PLC inatarajia kupokea maombi mengi ya kununua hisa katika kipindi cha wiki hii.
“Pia kutokana na ushauri kutoka serikalini na makundi mbalimbali muhimu ya kijamii yanayohitaji kuwekeza, wakiwamo wabunge, makundi ya watumishi wa kada mbalimbali wa serikali na maofisa wa vyama vya ushirika kutoka sehemu mbalimbali za nchi, tumewasilisha maombi na kupata idhini kutoka Mamlaka ya Soko la Mitaji na Dhamana (CMSA) kuongeza muda wa zoezi la kuuza hisa kwa kipindi cha wiki tatu hadi kufikia Alhamisi ya Mei 11, mwaka huu,” alisema Mworia.
Mkurugenzi huyo alisema kuongezeka kwa muda wa mwisho wa kununua hisa kutawezesha wanaohitaji kununua hisa kwa makundi binafsi na taasisi zilizoomba muda uongezwe kushiriki kikamilifu katika mchakato huo.
Alisema wanatoa shukrani kwa Watanzania ambao wamejitokeza kuwekeza kupitia kununua hisa na kuwakaribisha ambao bado hawajanunua kuchangamkia fursa hiyo katika muda huo wa nyongeza.
“Mgawanyo na mchanganuo wa umiliki wa hisa inapendekezwa utafanyika kuanzia Mei 19, mwaka huu na kuendelea kabla ya kumaliza mchakato wa mwisho wa kujisajili katika Soko la Hisa la Dar es Salaam katika tarehe iliyopangwa ya Juni 6, mwaka huu,” alisema. | 3 |
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amewatoa hofu wakazi 1,000 wa Manispaa ya Songea wanaodai fidia ya Sh bilioni 3.8 baada ya eneo lao kuchukuliwa na kugeuzwa kuwa la kiuchumi (Ruvuma SEZ) kwa ujenzi wa viwanda. Akizungumza mjini hapa jana na wakazi wa Kata ya Mwengemshindo katika mkutano wa hadhara, Majaliwa alisema Serikali inatambua kilio chao ambacho ni cha muda mrefu na alishawahi kupata ombi maalumu kutoka kwa Mbunge wao wa zamani, marehemu Leonidas Gama. “Alipotoka kutibiwa India alikuja ofisini kwangu na kunieleza kwamba ana mambo mawili ambayo nikifanya ziara mkoani Ruvuma anaomba niyatafutie ufumbuzi. La kwanza ni hili la fidia kwa wakazi wa Mwengemshindo na la pili ni la ujenzi wa kituo cha mabasi cha mjini Songea. “Leo (jana) nimefanya ziara maalumu kwa ajili yenu, kwa sababu Serikali iko kwa ajili yenu na hasa wananchi wanyonge. Na tatizo hili inalijua. Kabla sijafika hapa, nilipita kwenye eneo husika na ofisa mipango miji akanionyesha ramani ya eneo lenu hili,” alisema. Pia aliwaeleza wakazi hao kwamba eneo hilo limetengwa na manispaa kwa ujenzi wa viwanda na kwamba wawekezaji watatu tayari wamekwishajitokeza na wanataka kujenga viwanda vitatu. “Kutakuwa na kiwanda cha kusindika mahindi, kutengeneza pumba za kuku na ng’ombe na mbolea. Kiwanda cha pili kitakuwa ni cha kusindika kahawa na cha tatu kitakuwa ni cha kukamua mafuta ya mbegumbegu,” alisema na kuongeza kuwa reli ya kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay inatarajiwa kupita eneo hilo. Kuhusu kuchelewa kwa malipo hayo, alisema kati ya wawekezaji hao watatu, aliyekwishalipa fidia ni mmoja tu na kwamba kwa mujibu wa sheria ya uwekezaji, fidia inapaswa kulipwa na mnunuzi wa eneo husika. Hata hivyo, alikiri kuwapo kwa upungufu wakati wa ulipaji kwa sababu walifuata orodha ya majina (ki-alfabeti) badala ya kutoa malipo kwa wakazi wa eneo husika. “Sasa hivi mwekezaji anataka kuanza ujenzi, lakini ndani ya eneo lake kuna watu ambao bado hawajalipwa, kwahiyo hawawezi kutoka hadi wale waliobakia nao walipwe. Serikali itawafuatilia hawa wawekezaji wengine ili nao walipe fedha zao haraka ili waliobakia walipwe,” alisema. Jumla ya watu 2,179 walifanyiwa uthamini mwaka 2008 na gharama yao kubainika kuwa ni Sh 3,254,737,622. Juni 8-19, mwaka juzi, Serikali iliwalipa wakazi 1,179 jumla ya Sh 1,920,242,121 na kati ya hizo, Sh 1,210,078,261 zilikuwa ni malipo ya thamani ya mali za wananchi na Sh 710,163,860 zilikuwa ni riba kutokana na malipo hayo kuchelewa kufanyika. Katika hatua nyingine, Majaliwa alimwagiza Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Songea, Kundaeli Ndemfoo, afuatilie suala la bibi Monica Miti na watoto wake wanaodaiwa kudhulumiwa nyumba ya urithi na aliyekuwa mwanasheria wa manispaa hiyo. Alitoa agizo hilo katika mkutano huo baada ya kupokea bango lililoandikwa na bibi Miti kuomba arejeshewe umiliki wa nyumba ya marehemu mumewe. Alipopewa nafasi ya kueleza tatizo lake, bibi huyo aliyemtaja mwanasheria huyo kwa jina moja la Mwakasungura, alidai kuwa alighushi hati ya nyumba na kuwatoa ndani yeye na watoto wake. Alipotakiwa na Majaliwa aeleze alipo mwanasheria huyo, Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Tina Sekambo, alijibu kwamba alishahamishiwa Ukerewe. Majaliwa aliwaagiza Tina na Kundaeli wafuatilie suala hilo na wampe majibu mapema iwezekanavyo. Pia alimwomba bbi huyo na wanawe wafike kuonana naye Januari 3, mwakani atakapokuwa Songea kwa mapumziko mafupi ya mwisho wa mwaka. | 3 |
Aidha, serikali imeshauriwa kuangalia upya utaratibu wa kutoa misamaha ya kodi, hasa kwa kampuni kubwa zisizohitaji msamaha huo, kuwezesha kuongeza pato la Taifa kama Watanzania wanavyobanwa kulipa kodi katika mataifa ya nje waliomo.Hayo yalisemwa juzi na Mjumbe Kadari Singo, wakati akichangia mjadala wa Rasimu ya Katiba kuhusu Sura ya Kwanza na ya Sita.Akitoa mifano ya mataifa mengine, Singo alisema ripoti ya fedha ya mwezi wa pili mwaka huu ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), inaonesha kuwa Kenya inaingiza Dola za Marekani bilioni 1.7 kwa mwaka kutoka kwa Wakenya waliopo nje ya nchi hiyo.“Nigeria diaspora inaingiza Dola za Marekani bilioni 21 ambayo kwa hapa nchini, kiasi hicho cha fedha kinaendesha Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa miaka mitatu. Uganda zinaingia dola za Marekani milioni 910 na China ni dola za Marekani bilioni 60 kwa mwaka,” alisema Singo.Alisema Tanzania Diaspora inaingiza dola za Marekani milioni 10 hadi 37 kwa mwaka na kuwataka Watanzania kutopuuza raia walioko nje ya nchi, kwani wanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza uchumi.Singo alisema katika kuchangia katika pato la taifa, Uganda diaspora inachangia asilimia 4.3 wakati Lesotho inachangia asilimia 34.Alilitaka Taifa kufikiria kwa kina kuhusu uraia pacha na kueleza kuwa Tanzania ni moja ya nchi saba pekee Afrika, zinazokataa uraia huo.“Tusiwe wavivu kufikiria kuhusu uraia pacha, haki ya kuzaliwa kwa raia wa Tanzania walioko nje ni ya muhimu, viongozi wa Kitaifa wakija huko tuliko, tunawapokea na kuwazunguka kwa mazungumzo, leo tukija nyumbani tunaambiwa tumekimbia nchi, si kweli,” alisema Singo.HabarzotenaGloriTesha | 5 |
TAASISI mbalimbali na watu binafsi, wameonesha nia ya kumsaidia mwanafunzi, Yonana Lugedenga pamoja na familia yake, kumwezesha aendelee na masomo yake, baada ya kufaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza, licha ya mazingira magumu aliyosomea.Aidha, upande wa serikali, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka amesema mwanafunzi huyo ambaye ni tunda la mafanikio ya sera ya elimu bure, atapewa Sh milioni moja na kununuliwa vifaa vinavyohitajika, kujiunga na kidato cha tano, kama ilivyo kwenye mpango uliofikiwa na mkoa. Hata hivyo, Mtaka alisema jana kutokana na maoni na hoja mbalimbali, zilizotolewa kuhusu mwanafunzi huyo, katika tathimini watakayoifanya, wataangalia uwezekano wa kuweka pia mpango wa kufuatilia na kuwezesha wanafunzi wanaofaulu hadi chuo kikuu.Yohana ambaye amehitimu Shule ya Sekondari ya Igaganulwa Kata ya Dutwa wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, amefaulu mtihani wa kidato cha nne kwa kupata alama A masomo yote tisa. Mtaka alisema miongoni mwa taasisi ambazo zimewasiliana naye, zikitaka kumsaidia mtoto huyo ni Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), lililosema linataka kumsaidia.“Unesco wamenipigia simu, nadhani wanataka kum-support. Wana nia hata ya kusaidia wadogo zake…” alisema na kuongeza kuwa pia mkurugenzi mtendaji wa benki ya NMB na watu binafsi, waliowasiliana naye, walionesha kuwa wana jambo wanataka kulifanya.Akizungumzia matokeo na mjadala ulioibuka, kuhusu ufaulu wa Yohana aliyekuwa akisoma shule ya kata ya Igaganulwa, Mtaka alisema ni uthibitisho wa umma, kuanza kuamini shule za serikali.Alisema jambo ambalo umma haujafahamishwa ni kwamba mwanafunzi huyo, anamulika mafanikio ya sera ya elimu bure, iliyoanza kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk John Magufuli.“Hii ndiyo Form Four (kidato cha nne) ya kwanza tangu Rais Magufuli aingie madarakani. Kama isingekuwa elimu bure huyu mtoto angewezaje kusoma? Maeneo kama haya (vijijini) maisha yalikuwa magumu. Hata huyu mtoto asingeweza kusoma,” alisema Mtaka.Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga pia katika ukurasa wake wa Facebook, baada ya kumtembelea Yohana ambaye taarifa zinasema baba yake mzazi hayupo nyumbani tangu akiwa darasa la tano, alimshukuru Rais Magufuli kwa mpango wa elimu bure.Katika ukurasa huo wa Facebook, mkuu wa wilaya anaonekana katika picha tofauti akiwa na mama wa kijana huyo, Masalu Lulyalya pamoja na bibi yake, Mbuke Limbu na alisema, “Je isingekuwa elimu bure, ingekuwaje kwa watoto hawa kutoka familia masikini? Asante Dk Magufuli kwa maono ya hali ya juu kwa Watanzania hawa.”“Inatia hamasa sana na kumshukuru sana Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwa kuleta elimu bure. Maana taarifa ni kwamba kijana huyu hata uniform (sare) za shule kwa miaka yote alikuwa ananunuliwa na walimu wake kwa vile alijulikana kwa kuwa na akili nyingi sana”.Kulingana na mkakati wa mkoa, kuhusu watoto wa shule za serikali wanaofaulu kwa kupata alama 7 kwa maana ya A katika masomo yote kidato cha nne, hupewa Sh milioni moja za kukidhi mahitaji yake. Vivyo hivyo, kwa kidato cha sita kwa mwenye ufaulu wa alama 3.Kama angetajwa kuwa katika 10 bora kwa shule za serikali, angepata Sh milioni tatu ambazo huwekwa kwenye akaunti yake ya benki.“Shilingi milioni moja tunazotoa zinatimiza mahitaji. Kuhusu kufuatilia mwanafunzi hadi chuo, tulikuwa hatujafanya hilo. Tumepata uzoefu, matokeo yakitoka wengi wanajitokeza kusaidia. Katika tathimini ya mkoa hili tutaliangalia,” alisema Mtaka.Kwa mujibu wa Mtaka, mwaka jana pia mkoa wa Simiyu ulipata mwanafunzi aliyefaulu kwa alama 7 kutoka shule ya serikali. Alitoka Shule ya Sekondari ya kata ya Nkololo wilayani Bariadi. Akizungumzia kambi za kitaaluma, Mkuu wa Mkoa alisema zimekuwa na faida kubwa.Alisema mwaka 2016 alipofika Simiyu, katika mitihani yote ya kitaifa; darasa la nne, la saba, kidato cha pili, cha nne na sita, mkoa ulikuwa ukishika nafasi za 26,25 na 22.“Lakini leo katika mitihani yote, mkoa umeingia kumi bora. Utaona mwaka 2016 katika kidato cha nne tulikuwa wa 22, mwaka 2017 wa 14, mwaka 2018 wa tisa na mwaka 2019 tukawa wa tano. Wakati huo huo katika Darasala la Saba mwaka 2018 tulikuwa wa 22, mwaka 2019 namba tisa,” alisema Mtaka.Kwa mujibu wa Mtaka, mwaka jana, katika matokeo kwa shule za serikali, Simiyu iliingiza watoto wanne katika 10 bora na shule moja katika shule 10 bora. Mtaka alisema jambo ambalo linapaswa kuzingatiwa na serikali ni kutafuta namna ya kusaidia watoto, kuondokana na kusafiri umbali mrefu kwenda shule. | 3 |
Zari ambaye amezaa watoto wawili na Diamond, amewatangazia mashabiki wake kuachana na Diamond kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram.Alisema sababu ya kuamua kuchana na Diamond ni matukio mfululizo ya usaliti wa kimapenzi.Licha ya kuwa na Zari, lakini mara kadhaa Diamond amekuwa akikumbwa na kashfa za kutoka kimapenzi na wasichana wengine akiwemo Video Queen Tunda, na mwezi uliopita kuna msichana alisambaza picha ya video inayomuonyesha yuko Madale nyumbani kwa msanii huyo na alipoulizwa alidai kuitwa na kulala na msanii huyo.Mwaka jana aliingia kwenye kashfa ya kuzaa na mwanamitindo Hamisa Mobeto mtoto wa kiume, Abdul kabla ya kufikishana mahakamani kwa ajili ya matunzo ya mtoto huyo ambapo Diamond aliamuliwa kutoa fedha kila mwezi.Kana kwamba haitoshi, mwishoni mwa mwezi uliopita, Diamond alionekana na mpenzi wake wa muda mrefu Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu katika hafla ya kumtambulisha msanii mpya wa WCB Maromboso.Licha ya wawili hao kukanusha kwamba hawajarudiana, lakini mikao yao kwenye hafla hiyo ilizua maswali mengi. Zari aliandika ujumbe mrefu kwenye ukurasa wake juzi na kuweka wazi sababu za kuamua kuachana na nyota huyo aliyezaa nae watoto wawili, Latifa na Nillan.“Elewa hiki ni kitu kigumu sana kwangu kukifanya, kumekuwa na tetesi mbalimbali baadhi kati ya hizo zimekuwa na ushahidi ambao umekuwa ukisambaa katika vyombo vya habari kuhusiana na usaliti wa kimapenzi unaofanywa na Diamond, kwa huzuni nimeamua kuvunja uhusiano wangu wa kimapenzi na Diamond kwa heshima yangu”.“Tunaachana kama wapenzi lakini sio kama wazazi hii hainipunguzii mimi kuwa mtu wa kujitegemea, mama mwenye kujali na Boss Lady, wote mnatakiwa kufahamu hilo nitaendelea kujijenga kama mwanamke mwenye ushawishi, nitawahamasisha wanawake wote duniani kuwa maboss Ladies,”“Nitawafundisha watoto wangu wanne wa kiume kuwaheshimu wanawake na nitamfundisha binti yangu ni nini maana ya heshima, nimekuwa katika kiwanda cha burudani kwa miaka 12 sasa pamoja na changamoto zote hizo lakini nimefanikiwa kuwa mshindi kwa sababu mimi ni mshindi nawatakiwa wote siku njema ya wapendanao,” aliandika Zari.Baada ya ujumbe huo, mashabiki wa wawili hao walitoa maoni yao, wengine wakisikitika na wengine wakifurahi. Aidha mpaka jana mchana, Diamond hakuzungumza chochote kuhusu jambo hilo na waandishi wa gazeti hili walimsaka bila mafanikio.Kadhalika msanii huyo ambaye pia hupenda kutumia mitandao ya kijamii kuzungumzia masuala yake mbalimbali, jana hakuandika chochoe kuhusu tukio hilo na mpenzi wake huyo raia wa Uganda, zaidi ya kupost vitu vingine ikiwemo taarifa ya kundi lake la WCB kufungua tawi lingine Nairobi, Kenya kwa ajili ya kuendeleza vipaji. | 4 |
RIPOTI ya mwaka 2016 ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), ilibainisha kuwa watoto chini ya 18 zaidi ya milioni moja pamoja na wanawake milioni 3.8 ni waathirika wa ukahaba, unaohusishwa na Biashara Haramu ya usafirishaji wa Binadamu. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kati ya watu 10 wanaofanyiwa ukatili wa aina hiyo, 7 wanafanya shughuli za ukahaba katika Bara la Asia. Pia, ripoti ya mwaka 2017 ya shirika hilo, ilibainisha kuwa watu milioni 24.9 walikuwa wameingia kwenye biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu na zaidi ya asilimia 50 walikuwa wanatumikishwa kingono. Vilevile, takwimu za Global Slavery Index za mwaka 2018, zinabainisha kuwa Watanzania 336,000 wanatumikishwa kinyume cha haki za binadamu. Takwimu hizo pia zinaonesha kuwa kati ya watu 100 nchini, 60 wako kwenye hatari ya kuathirika kimwili au kiakili, kwa kutumikishwa kwenye masuala ya kazi, unyanyasaji wa kijinsia, ndoa za lazima na ukahaba. Hoja hiyo inaungwa mkono na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola wakati Wizara yake ilipokuwa inaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Biashara Haramu ya Us- afirishaji wa Binadamu, iliyo- fanyika hivi karibuni katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake, Waziri huyo alibainisha kuwa mkoa wa Dar es Salaam, unaongoza kwa biashara hiyo miongoni mwa mikoa saba vinara.Aliitaja orodha ya mikoa mingine nyuma ya Dar es Salaam kuwa ni Tanga, Kigoma, Mwanza, Shin- yanga, Singida na Dodoma, hususani Wilaya ya Kondoa. Waziri huyo alibainisha kuwa mbali na India, mabinti wa Tanzania wamekuwa wakisafirishwa kwenda kufanyishwa biashara ya ukahaba katika nchi za Thailand, Malasia na Indonesia.“Kuna baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Serikali ikiwa ni pamoja na kudhibiti utoaji wa hati za kusafiria, kuyafutia leseni makapuni yaliyokuwa yanawatafutia Watanzania kazi nchi za nje, kutoa elimu kwa vyombo vya utekelezaji wa sheria na umma kwa ujumla juu ya biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu na madhara yake,” alisema.Katika kukomesha biashara hiyo nchini, Waziri alisema, “Tunatarajia kuanza kufanya kampeni na ukaguzi nyumba kwa nyumba ili kuwatambua watu ambao ni wahanga wa biashara hiyo.”KAULI YASERIKALI YA INDIA Kamishna wa Polisi Kitengo cha Masuala ya Wanawake Jiji la Delhi, Aman Vihar, anakiri jiji hilo kuwa na idadi kubwa ya watu wanaojihusisha na biashara ya ukahaba na baadhi yao ni raia wa kigeni. Anasema Aprili 19, mwaka huu kitengo chake kilifanya operesheni ya kukamata wanaofanya biashara hiyo na kilibaini kuwa maeneo ya Aurobindo Marg, Green Park, Hauz Khas na Chattar Pur yaliyoko jijini humo, yamekithiri kwa biashara hiyo haramu.“Kwa kuwa kuna raia wa kigeni wanaojihusisha na biashara ya ngono, sisi tukishirikiana na Ofisi ya Uhamiaji ya Kanda (FRRO), atakayekamatwa anafanya biashara hiyo, ataondoshwa India mara moja,” Kamishna huyo anasema. Anasema India ina sheria kuhusu suala hilo. Anasema Sheria ya Udhibiti wa Usafirishaji Haramu wa Binadamu ya India ya mwaka 1956 Kifungu 3(i) inataja adhabu kwa atakayebainika kumiliki danguro au anaruhusu eneo lake kutumika kuendesha biashara za ukahaba kwa uwazi, kuwa ni faini na kifungo kisichopungua mwaka mmoja na kisichozidi miaka mitatu gerezani. “Kwa mujibu wa sheria yetu, biashara ya kuuza miili (ukahaba) ikifanyika mafichoni sio kosa kisheria nchini India, isipokuwa tu inakuwa kosa, pale iki- fanyika maeneo ya wazi. Ni kosa kushiriki kwenye vitendo vya uwakala wa ukahaba, ukuwadi na biasha- ra ya madanguro,”anaeleza Kamishna huyo. UBALOZI WANENA Balozi wa Tanzania nchini India, Baraka Luvanda, anasema kwa kipindi kirefu kumekuwa na tatizo la mamia ya mabinti wa Tanzania kuingia nchini humo na kujihusisha na biashara haramu ya ukahaba. Luvanda anasema wamekuwa wakijisalimisha ubalazoni hapo wanapokumbana na matatizo. “Idadi ya wanawake wa Kitanzania wanaofanya shughuli hizo hapa India inakadiriwa kuwa zaidi ya 300. Zamani walikuwa wengi zaidi, lakini Serikali ya Tanzania ilipoanza kuwadhibiti, idadi hiyo imeanza kupungua. Nawashauri wale waliopo nyumbani Tanzania, wasishawishike kuja India au kwenda nchi zingine kwa lengo la kufanya biashara za ukahaba kwa sababu ni haramu na hazina tija. Tanza- nia kuna shughuli nyingi za kufanya na za kuwaingizia kipato,” anasema. MASHARTI PASIPOTIMsemaji wa Jeshi la Uhamiaji nchini, Ally Mtanda, pia anakiri kuwa tatizo la mabinti wa Tanzania kusafirishwa kwenda India na nchi zingine za Asia ni kubwa. Anasema baadhi ya mabinti hao, wamekuwa wakipitia nchi jirani kwenda katika nchi hizo za Asia, baada ya hatua kadhaa kuchukuliwa na Serikali ya Tanzania, kukabiliana na biashara hiyo haramu. “Jeshi letu la Uhamiaji linatambua matatizo yanayowakumba mabinti wa Kitanzania nje ya nchi na tumeshaanza kupambana kwa kudhibiti utoaji wa pa- sipoti, hasa kwa wanawake wa umri wa kati. Wanawake wa kundi hili wanapokuja kuomba pa- sipoti, tunapowahoji, wamekuwa wakikosa maelezo ya kujitosheleza juu ya wapi wanapokwenda na nini wa- nachokwenda kukifanya. Hatua hiyo ya kutaka sababu za kueleweka za kwanini mtu anataka kusafiri kwenda nje ya nchi, zimesaidia kupunguza malalamiko na matatizo yaliyokuwa yakiripotiwa kufanywa dhidi ya Watanzania katika nchi za India, Falme za Kiarabu na nchi zingine za Bara la Asia. Kama anaenda kusoma, basi tutaona uthibitisho huo, kama ni kazi, tunataka kuona mkataba wa kazi wa zaidi ya miezi sita, lakini pia kwa yeyote anayetoka, lazima awe na tiketi ya kwenda na kurudi,” anafafanua Mtanda. UTAFITI, AJIRA Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa), Joyce Shebe, anasema biashara ya binadamu ni tatizo duniani kote.Anabainisha kuwa ni biashara haramu ya tatu katika biashara zinazowapatia wahalifu wa biashara hiyo faida kubwa sana. Biashara hiyo inatanguliwa na ile ya utengenezaji na uuzwaji wa silaha na kufuatiwa na uuzwaji wa dawa za kulevya. “Sisi wadau, serikali na balozi za Tanzania, tufanye utafiti, tuangalie tunatoko- meza vipi biashara hii haramu kwani ni udhalilishaji wa wanawake na ni kinyume cha haki za binadamu. Pia, jamii itambue kuwa kwenye biashara hii, wanawake wanawafanyia vitendo vya ukatili wan- awake wenzao kwa kuwauza maana wasimamizi wakuu wa biashara hii ni wanawake wenyewe,” anashauri. Kauli hiyo inaungwa mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi, ambaye pia anaona tatizo hilo linachagizwa na kutokuwapo kwa mfumo mzuri wa ajira na elimu katika nchi nyingi za kiafrika. “Kutokana na kutokuwa na mfumo huo mzuri wa ajira na elimu, wasichana au vijana wetu wamekuwa wakirubuniwa kirahisi kwenda nje ya nchi kutafuta ajira na mwisho wa siku wanaishia kudhalilishwa,” anafafanua. KAULI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikia- no wa Afrika Mashariki, Emmanuel Buholela, anasema kuwa kuna idadi kubwa ya raia wa kitanzania wanao husishwa na biashara hiyo wanapatikana katika miji mikubwa ya ya New Delhi, Bangalore, Mumbai, Hyder- abad, Goa na mingineyo. Anasema, “Idadi ya watanzania waliopo nchini India wakijihusisha na bi- ashara haramu za ukahaba na usafirishaji wa madawa ya kulevya kwa sasa kwa kipindi cha mwaka 2017 ilikuwa inakadiriwa kufikia 250 hadi 300.“Kwa sasa, baada ya jitihada za udhibiti wa uondokaji katika mipaka mingi ya Tanzania, zoezi la ubadilshaji wa pasi za kusafiria za Tanzania na pia jitihada zilizofanywa na Ubalozi kupitia mahojiano katika televisheni za Tanzania na machapisho mbali mbali, idadi ya watanzania hao imepungua,” anasema. Kwa ushahidi wa janga hilo, Buholela anasema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia Januari 2017 hadi Oktoba 2019 jumla ya hati za dharura za kusafiria 103 zilitolewa na Ubalozi, kuwasaidia baadhi ya wasi- chana hao kurejea nyumbani. Kwamba walisaidiwa baada ya kubainika kuwa waliku- wa wamenyang’anywa hati zao za kusafiria na madalali wa biashara hiyo haramu, ambao ndio walikuwa wamewapeleka nchini India. “Serikali inaendelea kusisitiza na kuwatahadharisha mabinti na vijana wote, wenye nia ya kwenda nje ya nchi hususan nchini India na kwingineko huku wakiwa hawajui wanachokwenda kufanya kuacha mara moja. “Wasirubunike au kuingia katika mtego wa wahalifu hao, kwa kuwa hakuna kazi kama wanavyoahidiwa.India ni nchi ya pili duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watu, ina takribani bilioni 1.2 baada ya China na mfahamu kwamba India nayo ina changamoto ya kuwa na idadi kubwa ya watu ambao wengi wao hawana ajira au fursa za kumudu ugumu wa maisha “Hivyo Serikali inawataka vijana kutafuta shughuli za kufanya ndani ya nchi na kujitengenezea ajira, badala ya kujiingiza katika biashara haramu za ukahaba na usafirishaji wa madawa ya kulevya,” anasema Buholela. Aidha, anaongeza kwa kusema kuwa Serikali ya Tanzania, inaendelea kuhimiza udhibiti wa mipaka kwa pamoja ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kwa kuwa mpaka mmojawapo unapokuwa na udhibiti duni, basi unakuwa | 3 |
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri amesema kama mkoa huo hautapata maendeleo ya kiuchumi wakati huu wa Serikali ya AwamuTano basi usahau habari ya maendeleo.Mwanri amesema mjini Tabora kuwa, haiwezekani mkoa huo wenye sifa kubwa kihistoria ukabaki masikini, na kwamba, watu mkoani humo wakiendelea kuishi maisha duni wa kulaumiwa si wananchi bali viongozi kwa kuwa watakuwa wameshindwa kuwaonyesha njia.“Tusikae hapa tunaabudu mambo ya ajabu ajabu, mambo ya ushirikina tuachane nayo, tumfuate Mungu, tumtafute Mungu alipo, tusiamini ubinadamu tu, Tabora we can, tunaweza…“Tabora, Tabora, Tabora sisi tunaweza, tuna akili, maprofesa wakubwa walitoka Sikonge, walioongoza nchi, wanaoongoza nchi wote walisoma Tabora”amesema Mwanri na kuongeza kuwa, mkoa huo unakwenda Jerusalem mpya, nchi ya ahadi yenye asali na maziwa.Amesema, hakuna mwanadamu asiye na akili, na kwamba, tofauti ya akili baina ya watu ipo kwenye matumizi tu.Amewataka wananchi wa Tabora wabadilike kifikra na waamini kwamba wanaweza kupata mafanikio kiuchumi na watambue kwamba, fursa hazitolewi, zinachukuliwa.“Na leo nataka niiambie Tabora yes we can na itakuwa, semeni yes we can, semeni yes we can, ndio tunaweza, Tabora nina uhakika kwamba tunaweza…come on Tabora, Tabora ni taa bora ” amesema Mwanri wakati wa mkutano wa wadau wa Jukwaa la Fursa za Biashara Tabora linalotarajiwa kufanyika Novemba 21 hadi 23 mjini Tabora.Katika mkutano huo kwenye ukumbi wa Chuo Cha Chuo Kikuu Cha Askofu Mkuu Mihayo (AMUCTA) Mwanri amesema, anataka wananchi mkoani huo wawe sehemu ya ujenzi na wanufaika kwa uchumi badala ya kulalamika na kuwa watazamaji tu.“Tunataka kila mmoja wetu katika Mkoa wa Tabora aseme mimi nitafanya nini ili na mimi niweze kushiriki katika jambo hili. Asiwe ni mtu tu mtazamaji. Tusije tutakawa ni watu wa kulaumu tu, nakusubiri mtu akusaidie tu, tunaye dereva tunayemkubali yupo juu pale Dk. John Pombe Magufuli ambaye ameamua kwamba aivushe nchi, habari hii ni ya sasa na wala sio kesho, it is now or never” amesema Mwanri.Amesema, Tabora inapaswa kujiandaa kwenda kwenye uchumi mpana zaidi na kwamba, hakuna muda wa kusubiri.“Wakati ni huu, wakati wa kunyanyuka Tabora ni huu, Tabora lazima inyanyuke, lazima tunyanyuke…tumkabidhi Mungu mambo yetu yote, Mungu anajua na asiyefanya kazi na asile...“Watu wa Tabora nawaomba, nawaomba kwamba nilimuomba Mungu nikamuomba Mungu nikamwambia Mungu nakushukuru umekubali niwe Mkuu wa Mkoa wa Tabora, ninakuomba ninapokuwa pale mkoa wa Tabora nikawe neema na baraka kwa watu wa Tabora, sema amen...“Ninakuje hapa nakaa na nyinyi miaka mitano napiga miayo tu, na wakati huo nawaacha mnapiga miayo. Mungu anapomtafuta mtu wa kumtumikia hamtafuti mtu mwenye akili, mwenye hela, anamtafuta mtu ambaye yupo tayari, mtu ambaye atatekeleza kusudi la Mungu la kumweka hapa duniani” amesema Mwanri. | 5 |
NA ABDUCADO EMMANUEL, DAR ES SALAAM LAZIMA wakae! Hizo ndizo tambo za mashabiki, makocha wa timu za Azam na Yanga kuelekea mchezo wao wa kuwania Ngao ya Jamii utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam saa 10.00 leo jioni. Mchezo huo wa aina yake ni kwa ajili ya kufungua pazia la Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2015/16, utakaoanza rasmi Septemba 12, mwaka huu. Kocha Mkuu wa Azam, Mwingereza Stewart Hall, amesema kuwa anataka kuendeleza rekodi yake ya kutwaa mataji mfululizo kwa kuifunga Yanga leo na anaamini ya kuwa kikosi chake kimeiva kutimiza kazi hiyo. “Wachezaji wangu wanapenda mechi kubwa kama hizi, Yanga ni timu kubwa tunaiheshimu, natarajia mchezo mgumu lakini naamini morali tuliyokuwa nayo itatimiza malengo tuliyojiwekea,” alisema. Naye Kocha wa Yanga, Hans van Pluijm, raia wa Uholanzi, amesema kikosi chake kimeimarika tofauti na kile kilichoshiriki Kombe la Kagame, hivyo anatarajia makubwa kwa timu yake. “Huu mchezo utakuwa tofauti na ule tuliocheza kwenye Kagame, kikosi changu kipo vizuri sana, nadhani utakuwa mchezo mzuri kutokana na ubora wa timu zote, ila tumejipanga kushinda,” alisema. Katika kujiandaa na mchezo huo, Azam iliweka kambi ya wiki moja Zanzibar, huku Yanga nayo ikitumia siku nane kujinoa vilivyo jijini Tukuyu, Mbeya. Ikiwa Zanzibar, Azam ilicheza mechi tatu za kirafiki na kushinda zote dhidi ya KMKM (1-0), Mafunzo (3-0) na JKU (2-0), Yanga nayo vivyo hivyo ikizifunga Kimondo (4-0), Prisons (2-0) na Mbeya City (3-2). Timu zote mbili zitaingia uwanjani zikiwa na hasira ya kulipizana kisasi, Yanga ikitaka kulipa kisasi cha kutolewa kwenye Kombe la Kagame dhidi ya matajiri hao kwa mikwaju ya penalti 5-3. Azam nayo itataka kulipa kisasi cha kufungwa mara mbili mfululizo na Yanga kwenye Ngao ya Jamii, iliichapa bao 1-0 mwaka juzi na mwaka jana ikainyuka 3-0, mchezo uliomng’arisha Mbrazil Geilson Santos Santana ‘Jaja’, aliyefunga mawili. Lakini Azam bado inashikilia rekodi ya kutisha tokea iliposhiriki Kombe la Kagame hadi kutwaa ubingwa huo, mpaka sasa haijafungwa kwenye mechi 13 mfululizo, ikiruhusu mabao mawili chini ya Hall na mechi 12 mfululizo bila wavu wake kuguswa. Yanga yenyewe imecheza mechi 12, imeambulia ushindi mara tisa, sare moja na vipigo mechi mbili, ikiwa imeruhusu kufungwa mabao sita. Ni wazi ya kuwa leo itakuwa ni vita kati ya mfumo wa 3-5-2 unaotumiwa na Azam uliowapa mafanikio makubwa sana ndani ya muda mfupi na ule wa 4-4-2 anaoutumia Kocha Pluijm wa Yanga. Timu zote mbili zipo vizuri langoni, Yanga ikiwa na mkongwe Ally Mustapha ‘Barthez’ na Azam inaye kinda anayetikisa, Aishi Manula, ambaye alidaka penalti ya Mwinyi Haji, iliyoiondoa Yanga katika Kagame. Azam ina mabeki bora zaidi wa kati wakiongozwa na Pascal Wawa na Agrey Morris, Yanga nayo imeimarisha eneo hilo kwa kumsajili beki Mtogo, Vincent Bossou, ambaye huenda akaanza na Kelvin Yondani ama Nadir Haroub au Mtogo huyo akasugua benchi kuwapisha wazoefu wa mechi hiyo. Bado timu zote zinatakiwa kuwa makini sana kwenye eneo la ushambuliaji kutokana na takwimu kuonyesha wanakosa mabao mengi ya wazi. Azam chini ya nahodha John Bocco, Kipre Tchetche, Shomari Kapombe na Farid Mussa (Wingbacks) kwenye eneo la ushambulizi, wameonyesha ubora, lakini wanakosa mabao mengi sana mchezoni. Hata Yanga yenye Amissi Tambwe, Donald Ngoma, Malimi Busungu, Deus Kaseke, nayo imekuwa vivyo hivyo, wanatengeneza nafasi nyingi bila kuzitumia vema. Mpira ni mabao. Hivyo utakuwa ni mchezo wa mbinu nyingi na sidhani kama tunaweza kushuhudia idadi kubwa ya mabao kama wengi wanavyotarajia kutokana na ubora wa pande zote. Kiungo cha Yanga kinaweza kuwa na Thabani Kamusoko, atakayecheza sambamba na Haruna Niyonzima, Salum Telela na Mbuyu Twite kama Said Juma atakuwa hayuko fiti. Hivyo watakuwa na vita kubwa dhidi ya wale watano wa Azam, Jean Mugiraneza “Migi’, Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Himid Mao, Farid na Kapombe, wanaocheza pembeni. Migi na Himid wamekuwa bora sana kuilinda safu yao ya ulinzi isifikiwe kirahisi iwe kushoto, kulia na katikati. Uimara wao na safu ya ulinzi pia ndio umechangia mafanikio yao mpaka sasa. Yeyote atakayemzidi mwenzake kwenye eneo hilo, basi ana nafasi kubwa ya kuibuka kidedea. Rekodi nyingine Kihistoria timu hizo zimekutana mara 14 kwenye ligi (misimu saba tokea Azam ipande), zote zimeshinda mara tano na sare nne kila mmoja, lakini Wanajangwani hao wamefunga mabao 20 na wapinzani wao 19. Yanga ina ukame wa mechi tatu sawa na dakika 270 za kushindwa kuifunga Azam, mechi ya mwisho iliifunga Septemba 14 mwaka jana, ikishinda mabao 3-0 kwenye Ngao ya Jamii. | 4 |
Sasa kumekucha rasmi baada ya Ratiba ya Ligi Kuu nchini England maarufu kama EPL kutangazwa hii leo. Ratiba hiyo inaonesha kwamba pazia litafunguliwa rasmi Ijumaa ya Agosti 9 mwaka huu ambapo Mabingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Liverpool watakuwa nyumbani Anfield kuwakaribisha Norwich City. Jumamosi, Agosti 10, michezo mingine itaendelea, ambapo West Ham watawakaribisha Mabingwa Watetezi Manchester City huku AFC Bournemouth wakiwa nyumbani kuwaalika Sheffield United. Mechi ni nyingine ni Burnley watakuwa maskani yao kuwakaribisha Southampton, Crystal Palace dhidi ya Everton, Leicester City watakumbana na Mbweha Wolves, Watford watawakaribisha Brighton Hove & Albion. Tottenham Hotspur watakuwa nyumbani kupepetana na Aston Villa ambao wamepanda daraja mwaka huu baada ya kukosekana misimu kadhaa katika Ligi Kuu ya England. Jumapili kutakuwa na patashika nguo kuchanika, ambapo watakuwa nyumbani kuwakabili Arsenal na mechi kubwa kuliko zote kwa wiki hiyo ya ufunguzi itakuwa katika Uwanja wa Old Trafford, ambapo Mashetani Wekundu Manchester United wataumana vikali na Wababe kutoka Darajani, Chelsea ‘The Blues’ | 4 |
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amewaagiza viongozi wa Jiji hilo kukamata mifugo yote inayozurura hovyo makazi ya watu na kuwatoza faini wamiliki.Aliagiza hayo baada ya kukutana na makundi ya ng’ombe wakizagaa hovyo kwenye makazi ya watu kwenye mitaa jijini humo wakati akiwa kwenye ziara ya kukagua ujenzi wa madarasa.Alisema hivi sasa Dodoma ni Jiji linatakiwa kuwa safi na mazingira yake kutunzwa bila kuharibiwa na mifugo, hivyo viongozi wa jiji wanatakiwa kuhakikisha hakuna mifugo inayofugwa hovyo katika makazi ya watu.“Kama kuna mtu anataka kufuga mifugo lazima awe na banda la kulishia mifugo hiyo ndani, badala ya ufugaji huo wa kutembeza mifugo hiyo kwenye makazi ya watu,” alisema.Alisema ni marufuku kuendesha ufugaji wa mifugo katika makazi ya watu, barabarani na maeneo mbalimbali kwani linatakiwa kuwa safi.Dk Mahenge alimtaka Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Petrobas Katambi kukamata mifugo na kuwatoza faini wanaofugia makazi ya watu kwa kutumia sheria ndogo za halmashauri ya Jiji zinazoruhusu kukamata mifugo na kuchukua hatua dhidi ya wanaofugia makazi ya watu.Mkuu wa Wilaya, Katambi aliyekuwa na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Hidaya Maeda waliahidi kutumia sheria ndogo kuwachukulia hatua wale wote wanafugia mifugo katika makazi ya watu.Katambi amesema wanalichukulia agizo hilo la Mkuu wa Mkoa kwa uzito mkubwa na hivyo watatumia sheria ndogo katika kukamata mifugo yote inayofugwa makazi ya watu. | 3 |
UFARANSA imesema ina imani kubwa na safari ya Tanzania kwenda kwenye uchumi wa kati kupitia viwanda mwaka 2025 kutokana na kasi ya ukuaji wa uchumi wake.Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Balozi wa nchi hiyo hapa nchini, Frederic Clavier alisema kutokana na hali hiyo wawekezaji wa Ufaransa wameona haja ya kuja Tanzania.“Ufaransa ina imani kubwa na maendeleo ya Tanzania na kampuni za Kifaransa hazina mashaka katika kuja kuwekeza hapa na kufanya biashara na Watanzania kila zinapokotokeza fursa hizo,” amesema Balozi Clavier.Alisema biashara kati ya nchi hizo mbili imeongezeka kwa asilimia 30 kwa mwaka jana sawa na dola za Marekani 200.Balozi Clavier alisema katika kuisaidia Tanzania kukuza uchumi wake na pia kuimarisha ushirikiano, jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania na wa Ufaransa wanatarajiwa kukutana hivi karibuni.Kwa upande mwingine, alisema Shirika la Maendeleo la nchi hiyo (AFD) limeahidi kuongeza misaada yake kwa Tanzania mpaka kufikia dola milioni 110 katika miradi ya maendeleo katika sekta ya maji, usafirishaji na umeme pamoja na ahadi nyingine ya dola milioni 23. | 5 |
KARIBU asilimia 80 ya wananchi waishio Tanzania Bara hawasajiliwa wala kuwa na vyeti vya kuzaliwa, huku wale waliosajiliwa na kuwa na vyeti hivyo wakiwa ni asilimia 13.4.Hayo yalibainishwa juzi mjini hapa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Emmy Hudson. Alikuwa kwenye ufunguzi wa semina ya viongozi wa wilaya na mkoa wa Singida ya usajili wa vizazi kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano unaotarajiwa kuanza kutekelezwa Machi mwaka huu katika mikoa ya Singida na Dodoma.Alisema kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya mwaka 2012, ni asilimia 13.4 tu ya wananchi wa Tanzania Bara ambao wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa, huku asilimia 86.6 wakiwa hawana vyeti hivyo. Emmy ambaye pia ni Kaimu Kabidhi Wasii Mkuu, alieleza kuwa kutokana na hali hiyo, Tanzania sasa ni moja ya nchi zenye kiwango cha chini sana cha usajili barani Afrika.Aidha, alieleza kuwa tayari maboresho ya jumla ya mfumo mzima wa usajili yameanza kufanyika chini ya Mkakati wa Kitaifa wa kuboresha Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu na Takwimu (CRVS) ulioandaliwa baada ya kufanya tathmini ya kina kubaini changamoto za mfumo wa usajili uliopo. Alisema katika tathmini iliyofanyika maeneo mbalimbali nchini, RITA ilibaini baadhi ya sababu za wananchi wengi kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa kuwa ni umbali uliopo kati ya maeneo ya makazi ya wananchi hadi Ofisi za Wakuu wa Wilaya kunakofanyika usajili.Pia uelewa mdogo juu ya umuhimu wa cheti cha kuzaliwa na kuwepo ada ya cheti. Alieleza kuwa Mpango wa Usajili wa Watoto walio na umri chini ya miaka mitano ambao hufanyika kwenye vituo vya tiba na ofisi za watendaji kata ambapo wahusika kusajiliwa na kupewa vyeti vya kuzaliwa papo hapo bila malipo, unatekelezwa kwa mafanikio makubwa katika mikoa 11 nchini.Mikoa hiyo ni Mwanza, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Geita, Shinyanga, Mtwara, Lindi, Mara na Simiyu. Akifungua semina hiyo ya siku moja, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi alisisitiza umuhimu wa kutekeleza mpango huo kwa ufanisi na umahiri, huku akisema kuwa usajili wa watoto ni jambo la lazima na ni thawabu kwa watekelezaji. Alionya watendaji wa dhidi ya ukiritimba, uhujumu au ukwamishaji wa mpango huo kwa kisingizio chochote kile huku akiitahadharisha RITA kutokuwa moja ya wakwamishaji wa shughuli hiyo kwa kuchelewesha kupeleka vitendea kazi maeneo husika. | 3 |
Ramadhan Hassan-Dodoma Wizara ya Afya, Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na Wazee na Watoto imesema mpaka sasa watu wanne wamefariki
kutokana na Homa ya Ugonjwa wa Dengue. Akitoa kauli ya Serikali bungeni leo June 21, Waziri wa Wizara hiyo, Ummy Mwalimu amesema kwamba jumla ya watu wanne wamefariki kutokana na ugonjwa huyo ambapo kwa Mkoa wa Dar es salaaa wamefariki watu watatu na Dodoma mmoja. Waziri Ummy
amesema jumla ya wagonjwa 4,320 na vifo 4 vimetolewa taarifa huku Mkoa wa Dar
es salaam ndio ukiwa kinara kwa kuwa na wagonjwa wengi. “Mkoa wa Dar e salaam una wagonjwa 4,029 na vifo vitatu, Dodoma wagonjwa watatu na kifo kimoja, Tanga wagonjwa 207 kifo hakuna, Pwani 57 hakuna kifo, Morogoro 16 hakuna kifo, Arusha watatu hakuna kifo, Singida wawili hakuna kifo, na Kagera wawili hakuna kifo,” amesema. Aidha amesema kuwa takwimu za hali ya maambukizi ya ugonjwa wa Dengue zinaonesha kuwa maambukizi mapya yamepungua kutoka wagonjwa 2494 kwa mwezi Mei 2019 hadi wagonjwa 813 kufikia tarehe 19 Juni 2019. | 3 |
AVELINE KITOMARY SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imetoa wito kwa wafanyakazi wa saluni kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (Covid-19) kutokana na kundi hilo kuwa katika hatari kubwa ya maambukizi. Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Kitengo cha Maji na Usafi wa Mazingira, Wizara ya Afya, Anyitike Mwakitalima, wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga na virusi hivyo. Mwakitilima alisema licha ya kundi hilo kuwa katika hatari, pia lina uwezo wa kuwaambukiza watu wengine wakiwamo wateja wao. “Kwa wale ambao wanasafisha nywele, kucha, wanafanya ‘massage’, wanaosuka nywele, mchukue tahadhari kwa sababu mpo katika hatari kubwa sana ya kuambukizwa, lakini vile vile kuambukiza watu wengine maambukizi ya virusi vya corona,” alisema Mwakitalima. Alisema Serikali inaendelea kuwakumbusha wafanyakazi wote katika maeneo ya saluni kuhakikisha wanaepuka msongamano pindi wanapokuwa katika majukumu yao, huku akisisitiza ni muhimu kwa kinyozi kuvaa barakoa pindi anaponyoa. “Tunawakumbusha, tena kwa upendo kabisa, tunawakumbusha muepuke msongamano, ndani awepo mtu anayenyoa na anayenyolewa, na yule ambaye ananyoa ahakikishe muda wote amevaa barakoa, tunawaambia hivi kwa sababu tunawapenda,” alisema Mwakitalima. Kwa upande wake, Sfaff sergeant (S/Sgt) Valentine Ngowi, aliwataka madereva wote wa vyombo vya moto, hususan bodaboda na bajaj kuhakikisha wanavitakasa vyombo vyao vya usafiri kwa sabuni mara kwa mara ili kuua maambukizi ya virusi vya corona endapo vitakuwepo. “Kwa madereva hasa wa bodaboda na bajaj wahakikishe wanajikinga kwa kutakasa vyombo vyao kwa maji na sabuni mara kwa mara ili kujiweka salama zaidi dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona,” alileza Ngowi. Naye balozi wa kampeni ya Mikono safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) amesisitiza kuwa ili kupambana na corona, watu wasichoke kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka ili kuepuka kupata maambukizi. Uhamasishaji huu unaofanywa kupitia kampeni hii ya “Mikono safi, Tanzania salama” inayoratibiwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Project CLEAR kwa kushirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery unaendelea katika Jiji la Dar es Salaam. | 3 |
Na Abdallah Amiri, Igunga BAADHI ya wanawake Wilayani Igunga mkoani Tabora waishio katika kaya masikini wameushukuru Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), kwa msaada wa fedha wanazopatiwa kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini. Mkazi wa Kata ya Igunga, Grace Matriga, ambaye ni miongoni mwa akinamama wanaonufaika na mpango huo alisema tangu afanikiwe kuingizwa katika mpango huo fedha ambazo amekuwa akipewa Sh 64,000 zimemsaidia kusomesha watoto wake shule. “Ninawatoto wanne Amani Gerald anasoma shule ya sekondari Mwayunge kidato cha nne Emmanuel Gerlad anasoma shule ya sekondari Igunga kidato cha kwanza huku Wilifrida Gerald na Witnes Gerald wakisoma chekechea Shule ya Msingi Igunga,” alisema. Alibainisha kuwa kabla hajaingizwa katika mpango huo wa TASAF alikuwa hana uhakika kama watoto wake wangeweza kuendelea na masomo lakini hivi sasa anamshukuru Mungu kuwepo kwa TASAF. “Fedha ninazopata nanaendelea kuzitumia kwa mahitaji ya wanafunzi ikiwamo sare za shule, madaftari sambamba na vitu vingine,” alisema. Kwa upande wake Mratibu wa TASAF Wilaya ya Igunga, Dina Madeje, amesema hadi sasa wanafunzi 5763 wa shule za msingi na sekondari pamoja na watoto wa chini ya miaka mitano 6,728 wanasoma shule na kupelekwa kliniki kupitia fedha za mfuko huo. Hata hivyo Madeje aliongeza kuwa zoezi la uhakiki kwa walengwa wa TASAF ni endelevu na kuongeza kuwa swala la kupeleka watoto shule na kliniki si la hiari bali ni lazima kwa kila mlengwa wa TASAF. | 3 |
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa orodha ya awamu ya pili yenye jumla ya wanafunzi 11,378 wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 35 kwa mwaka wa masomo 2019/20. Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru jana ilisema idadi hii ya awamu ya pili inafanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo kufika 42,053 na wamepata mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 148.56.Katika orodha ya awamu ya kwanza iliyotangazwa wiki iliyopita, wanafunzi wa mwaka wa kwanza 30,675 walipata mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 113.5.Badru alisema katika mwaka wa fedha 2019/2020, serikali imetenga Sh bilioni 450 kwa ajili ya jumla ya wanafunzi 128,285, kati yao wanafunzi zaidi ya 45,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza na wengine 83,285 ni wanafunzi wenye mikopo wanaoendelea na masomo. Mwaka 2018/2019, Sh bilioni 427.5 zilitengwa na kuwanufaisha jumla ya wanafunzi 123,285 wakiwemo wanafunzi 41,285 wa mwaka wa kwanza. “Tumeboresha sana mifumo yetu na sasa mwanafunzi anaweza kufungua akaunti yake aliyoombea mkopo maarufu kama Student’s Individual Permanent Account (SIPA) na kupata taarifa zake zikiwemo za kiwango cha mkopo alichopata,” alisema Badru. Pamoja na SIPA, Badru alisema majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo katika awamu hii ya pili yanapatikana katika mtandao wa HESLB wa uombaji mkopo (https://olas.heslb.go.tz) na tovuti ya Bodi (www.heslb. go.tz). “Bodi inapenda kuwasihi waombaji wa mikopo kuwa watulivu wakati mchakato wa upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye sifa kwa awamu inayofuata ukiendelea,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo | 3 |
Na MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM RAIS Dk. John Magufuli amemng’oa Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru na nafasi yake kurithiwa na Dk. Osward Mashindano. Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu jana usiku, ilieleza kuwa Dk. Mashindano anachukua nafasi hiyo na Mafuru atapangiwa kazi nyingine. Mafuru, hivi karibuni aliibuka na kauli tata ambayo ilionekana kupingana na Rais Magufuli kuhusu uamuzi wa baadhi ya taasisi za umma kuweka fedha katika Fixed Deposit Accounts (akaunti maalumu). Kauli hiyo aliitoa Novemba 30, mwaka huu katika mahojiano maalumu na redio moja nchini. Alisema haiwezekani kwa watumishi wa umma kuiba fedha zinazowekwa katika Fixed Deposit Accounts kwa sababu miamala ya benki ni ya uwazi. Alisema hizo ni tuhuma tu na Serikali imemwagiza CAG kuchunguza. “Nimefanya kazi katika taasisi za benki kwa miaka 20, sijawahi kuona watumishi wa umma wakichota hela kwenye fixed deposit account. “Pale kwenye benki kuna miamala ya aina mbili tu, ya kuweka na kutoa. Usipoweka wazi wakati wa kuweka, siku utakapozitoa itaonyesha tu,” alisema Mafuru. Alisema hakuna kosa kwa taasisi za Serikali kuweka fedha katika akaunti hizo, lakini Serikali sasa imeamua kuzihamishia Benki Kuu (BoT) ili iwe rahisi kuzifuatilia. Kauli hiyo ya Mafuru ilitanguliwa na ile ya Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu, ambaye alisema si kosa kisheria kwa taasisi kufungua akaunti maalumu katika benki ya biashara. Novemba 26, mwaka huu, Rais Magufuli alifichua siri ya hatua yake ya kuitumbua Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Alisema alilazimika kuchukua hatua hiyo baada ya bodi hiyo kuidhinisha Sh bilioni 26 kupelekwa kuwekwa katika akaunti maalumu (Fixed Account) katika benki kadhaa za biashara. Bodi hiyo ilitoa idhini ya kupelekwa fedha hizo katika benki hizo wakati kuna agizo la Rais la kupiga marufuku taasisi za umma, mashirika ya umma, idara za Serikali, wakala na wizara kuweka fedha zao katika benki za kibiashara. Fedha hizo zinatakiwa zifunguliwe akaunti BoT. Hatua hiyo ilitokana na uamuzi wake wa kuvunja Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, na saa chache akateua Naibu Kamishna Mkuu mpya. Ikulu bila kueleza sababu, ilisema kwamba Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, Bernard Mchomvu na kuivunja bodi nzima. Aidha, pamoja na kuivunja bodi hiyo, alimteua Charles Kichere kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, kuziba nafasi iliyokuwa wazi kwa mwaka mmoja baada ya Dk. Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa akishikilia wadhifa huo, Lusekelo Mwaseba. Akihutubia katika mahafali ya 31 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Makao Makuu ya chuo hicho, Bungo wilayani Kibaha mkoani Pwani, Dk. Magufuli alisema aliitumbua bodi hiyo kutokana na kukiuka taratibu. Alieleza kuwa kitendo chao cha kuidhinisha fedha hizo kuwekwa katika benki tofauti, ni tofauti na maelekezo kwani huo ndio ulikuwa mchezo unaofanywa na taasisi na mashirika mbalimbali. Rais Magufuli alisema kumekuwa na mchezo wa wakuu wa taasisi mbalimbali kuchukua fedha na kuziwekwa kwenye akaunti maalumu ambako serikali inakwenda kukopa kwa gharama kubwa. MABADILIKO Rais Magufuli pia amefanya uteuzi wa katibu mkuu mmoja na mkuu wa mkoa mmoja na mabadiliko madogo katika wizara na mikoa. Amemteua Profesa Faustin Kamuzora kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais. Kabla ya uteuzi huo, alikuwa Katibu Mkuu Mawasiliano. Rais Magufuli amemteua pia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew Mtigumwe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo anayeshughulikia Kilimo akichukua nafasi ya Dk. Frolence Turuka aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Dk. Turuka anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Job Masima ambaye ameteuliwa kuwa balozi. Rais Magufuli amemteua Dk. Maria Sasabo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na atakuwa akishughulikia mawasiliano, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Kamuzora ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais. “Pia Rais Magufuli amemteua Mhandisi Angelina Madete kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Maria Sasabo aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano “Aidha, Rais Magufuli amemteua Dk. Aloyce Nzuki kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,” ilieleza taarifa hiyo. SENDEKA AONDOLEWA CCM Mbali na uteuzi huo Rais Magufuli, amemteua Msemaji wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Christopher ole Sendeka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe. Sendeka anachukua nafasi ya Dk. Rehema Nchimbi ambaye amehamishwa kituo cha kazi na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida. | 3 |
Na MWANDISHI WETU-CONGO TIMU ya soka ya Yanga jana ilikubali kipigo cha mabao 3-1 dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika uliochezwa Uwanja Stade du TP Mazembe, nchini Congo. Matokeo ya jana yaliiwezesha TP Mazembe iliyokuwa imefuzu hatua ya nusu fainali kufikisha pointi 13 katika Kundi A, huku Yanga ikiondoshwa kwenye michuano hiyo ikiwa imejikusanyia pointi nne. Hata hivyo, Waarabu wa Algeria, Mo Bejaia walichomoza na ushindi wa bao 1-0 nyumbani na kufikisha pointi nane sawa na Medeama ya Ghana lakini ikayaaga mashindano. Pamoja na kipigo cha bao 1-0 walichokipata jana, Medeama imetinga hatua ya nusu fainali kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa. Katika mchezo wa jana, Mazembe iliandika bao la kuongoza dakika ya 28 kipindi cha kwanza kupitia kwa mshambuliaji wake, Jonathan Bolingi, aliyeunganisha pasi ya Deo Mukok. Bao hilo liliongeza kasi ya mashambulizi langoni kwa Yanga hali iliyosababisha mwamuzi, Helder Martins de Carvallo wa Angola kumwonyesha kadi nyekundu, Andrew Vicent ‘Dante’ wa Wanajangwani hao dakika ya 31 baada ya kumchezea vibaya mchezaji wa Mazembe. Mazembe walikwenda mapumziko wakiongoza kwa bao 1-0, lakini walianza kipindi cha pili kwa kasi na kuongeza bao la pili dakika ya 55 mfungaji akiwa ni Rainford Kalaba baada ya kupokea pasi safi ya Djo Issama Mpek. Dakika ya 64, Kalaba aliipatia Mazembe bao la tatu akimalizia kazi nzuri ya Mpek, kabla Yanga kuzinduka dakika ya 75 na kuandika bao la kufutia machozi kupitia kwa mshambuliaji wake, Amissi Tambwe. Bao la Yanga lilitokana na kazi nzuri iliyofanywa na mlinzi wa kushoto, Mwinyi Haji. | 4 |
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amezindua huduma za viza na vibali vya ukaazi vya kielektroniki na kuwataka watu wote watakaopewa vibali hivyo, kutii sheria kwa kufanya shughuli ambazo wameelekezwa kwa mujibu wa vibali vyao na si vinginevyo.Amesema utoaji wa huduma hizo ni miongoni mwa jitihada za serikali katika kuvutia uwekezaji, hususan katika sekta ya viwanda. Waziri Mkuu aliyasema hayo jana wakati akizindua huduma za viza na vibali vya ukaazi vya kielektroniki katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.Alisema kwamba hatua hiyo itasaidia kuondoa urasimu na ucheleweshwaji wa huduma na kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi. Kwamba pia itarahisisha upatikanaji wa vibali hivyo kwa raia wa kigeni na kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi. Alisema Idara ya Uhamiaji inatarajia kuanza kutoa huduma tajwa kwa raia wa kigeni muda wowote kuanzia sasa.Alisema kwa kupitia huduma hiyo, raia wa kigeni wataweza kuomba vibali hivyo kwa njia ya kielektroniki wakati wowote na mahali popote walipo. Waziri Mkuu alisema watakaopewa vibali, wanatakiwa kufanya shughuli zao kwa mujibu wa vibali vyao, kwa sababu kufanya shughuli tofauti na ilivyoainishwa kwenye kibali ni kosa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Uhamiaji.Alisema matumizi ya mtandao katika utoaji wa huduma za viza na vibali vya ukaazi ni hatua ya mfano, kwani inakwenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na teknolojia na sera ya serikali ya matumizi ya Tehama katika shughuli za serikali (e-government).Alisema serikali inatarajia kuwa matumizi ya mifumo hiyo, itaongeza ukusanyaji wa maduhuli ya serikali kwa kuwa mteja ataweza kulipia huduma hizo mwenyewe moja kwa moja pasipo kupitia kwa mawakala au mtu yeyote. “Natoa mwito kwa maofisa, askari pamoja na watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji kuhakikisha kuwa mifumo hiyo inatunzwa pamoja na kuendeleza miundombinu yote ya kiutendaji.” | 3 |
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuhakikisha inatia saini haraka Mikataba ya Upanuzi wa Lango la Bandari ya Dar es Salaam na ununuzi wa vifaa vya kupakia na kupakua mizigo.Alitoa agizo hilo wakati wa uzinduzi wa Gati namba 1 katika Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya upanuzi wa bandari hiyo ambapo hadi kukamilika itagharimu Sh bilioni 968.“Mhandisi Mshauri, Mkandarasi fanyeni kazi. Watanzania wanataka kuona kazi nzuri. Hawataki kuona maneno mazuri. “Mimi ni injinia sina maneno mazuri. Nakwenda moja kwa moja ili niweze kuhakikisha kwamba watanzania wengi, majirani zetu wengi Zambia, Kongo na wengine wanatumia Bandari ya Dar es Salaam,” alisema. Alitaka upanuzi wa lango la meli kuingia Bandari ya Dar es Salaam ufanyike haraka ili meli kubwa ziweze kutia nanga bandarini hapo.Gati namba 1 lililozinduliwa lina uwezo wa kupokea meli kubwa zinazoweza kubeba makontena 4,000 mpaka 6,000 kutoka makontena 200 hadi 2,800 awali. “Mkandarasi hakikisha kazi hii inakamilika kabla ya wakati ili bandari ihudumie watu wengi. Nataka Mkataba wa kukamilisha upanuzi wa Mlango wa Meli kuingia bandarini usainiwe katika muda wa miezi miwili ili Mkandarasi aanze kazi.Tuongeze kina na upana. Tunataka meli ziingie zishushe mizigo bandari ya Dar es Salaam,” alisema. Waziri Kamwelwe pia aliitaka TPA kununua vifaa vya kupakia na kupakua mizigo haraka ili kasi ya huduma za bandari hiyo iendane na upanuzi wake. “ Mhandisi Mshauri anatuchelewesha? Jamani si fedha tunayo. Tunayo iko kwenye akaunti sasa kwa nini hamuingii mkataba kununua vifaa.“Mniletee taarifa na programu, mikataba tunaingia lini, sitaki kusikia mwezi wa 11. Kwani ugumu uko wapi. Ni mwezi mmoja mikataba yote tuwe tumeingia. Watanzania hawa wanataka huduma.Nchi zinazotuzunguka zinahitaji huduma,” alisisitiza Waziri Kamwelwe. Pia alisema serikali imeanza ukarabati wa Bandari ya Tanga ili kuongeza kina. “Kwa sababu sasa hivi Bandari ya Tanga meli kubwa inasimama meta 1,400 kutoka bandarini kutokana na kina kidogo cha maji. Kina cha sasa ni mita 3 mpaka 4 kwa hiyo meli haiwezi kwenda moja kwa moja mpaka kwenye gati. Naibu Mkurugenzi Mkuu TPA, Augustine Phillipo alisema Gati namba 1 lilikamilika Desemba 2018 na lina urefu wa mita 191. | 3 |
WAWEKEZAJI sekta ya utalii katika kisiwa cha Pemba wametakiwa kuungana pamoja, kuieleza serikali vikwazo vya maendeleo ya sekta hiyo katika kisiwa hicho vinavyozuia wawekezaji wazawa kusonga mbele.Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) pia imeendelea na kampeni yake ya kushawishi wananchi wa Pemba kupokea sekta ya utalii na kuifanyia kazi kwa kasi kwa ajili ya maeneleo yao na taifa.Kauli hizo zimetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed wakati wa mahojiano na HabariLEO.Amesema, katika mahojiano hayo akijibu hoja za wenye mahoteli na nyumba za wageni kwamba sekta inakwazwa na tozo mbalimbali, Waziri Aboud amesema taratibu za utalii zinazofanyika Unguja ndizo zinazofanyika Pemba.Amesema sekta hiyo na tozo zake zinaakisi mfumo wa malipo uliokubalika nchini na Afrika Mashariki, lakini kama kuna kikwazo ni vyema wafanyabiashara hao wakaungana pamoja na kuleta hoja ili serikali ione inafanya nini.Wakati watalii Unguja wamefikia takriban 500,000 kwa mwaka 2018, kisiwa cha Pemba kimekuwa kikipokea wageni wachache zaidi ingawa taratibu ni zilezile zinazotumika Unguja.Baadhi ya wafanyabiashara waliohojiwa walisema kwamba wawekezaji wazawa wanakwamishwa na rundo la kodi na tozo na kwamba ingelikuwa vyema kama Pemba ingekuwa na utaratibu mwingine usiolingana na Unguja ambao tayari wameimarika kiutalii.Sehemu kubwa ya utalii wa Unguja ni wa mali kale ikiwamo majengo ya kale na mji Mkongwe wakati utalii Pemba unategemea zaidi maumbile japo nao wana fukwe njema na misitu ya kupendeza kama wa Ngezi.Hata hivyo wachache ambao wameweka vitega uchumi vyao wanalalamikia kiwango kikubwa cha tozo zinazochukuliwa na kamisheni ya utalii, kodi na tozo nyingine kwa kila mgeni anayelala wakisema kwamba kiwango ni kikubwa na kinawanyika fursa ya kukua.Moja ya tatizo kubwa katika sekta ya utalii Pemba ni ukosefu wa makazi ya kutosha kwa wageni.Hata hivyo waziri huyo amesema kwamba kama suala ni tozo ni vyema wafanyabiashara hao wakaketi pamoja na kuelezea vikwazo vya kukua kwa uwekezaji katika sekta ya utalii na kuwasilisha serikalini ili viangaliwe upya pamoja na mapendekezo yao hali iweje.Pamoja na kuhimiza kuwasilisha malalamiko yao, pia Waziri Aboud aliwataka wakazi wa Pemba ambao wamewekeza vitega uchumi vingi bara na Unguja kufanya kila linalowezekana kuwekeza Pemba ili kuinua uchumi kupitia utalii.Alisema utalii wa Pemba ni miongoni mwa utalii adimu duniani.Katika utalii huo watu wanapata nafasi ya kutembelea fukwe, kuangalia misitu na maumbile mbalimbali yanayovutia.Aidha kuna kisiwa cha Misali ambacho kina samaki wa aina mbalimbali wenye kuvutia na kina cha bahari kinachoruhusu upigaji mbizi wenye tija, kuona viumbe mbalimbali wa baharini.Kisiwa cha Pemba pamoja na kuwa na maumbile yanayopendeza, ni kisiwa chenye ukijani mkubwa na kinategemewa kwa kilimo kulisha Unguja.Waziri Aboud alisema ingawa serikali katika hilo inaona haja ya kuweka vivutio lakini ni vyema wafanyabiashara wenyewe wazawa kusema kitu wanachohitaji katika kuendeleza sekta ya utalii.Pamoja na kusikiliza kilio cha wafanyabiashara hao, waziri Aboud amesema kwamba kuna tatizo la mapokeo katika kisiwa hicho ambayo yanakwamisha kasi ya utalii.Alisema serikali inaendelea na kuhimiza jamii kukubali mabadiliko kuwezesha sekta ya utalii kukua na kuifaidisha jamii yenyewe na taifa kwa kuwa na wageni wengi wanaotembelea eneo hilo. | 5 |
KOCHA wa Azam FC Ettiene Ndayiragije amesema mchezo wa leo wa fainali Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati Kombe la Kagame ni wa kisasi.Akizungumzia mchezo huo jana kupitia sauti iliyotumwa na Msemaji wa klabu hiyo Jaffar Maganga, Ndayiragije alisema kwa kuwa mchezo wa kwanza wa makundi walipoteza 1-0 dhidi ya KCCA, hawatakubali tena iwe hivyo.“KCCA ni timu nzuri tulikutana nao hatua ya makundi tulikuwa bado hatujaunganika vizuri, tunawafahamu nina imani mechi itakuwa bora zaidi na sisi tunahitaji kulipiza kisasi,”alisema.Ndayiragije alikiri kuwa mchezo hautakuwa rahisi kwa kila mmoja kutokana na umuhimu wake, wakitaka kuweka historia ya kulichukua mara tatu mfululizo na KCCA wanataka kuweka historia ya kulitwaa baada ya kulikosa kwa miaka mingi. Mabingwa hao watetezi walifanikiwa kufika hatua hiyo baada ya kuitoa AS Maniema ya DR Congo kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya kucheza dakika 120 bila kufungana.Aidha, wapinzani wao KCCA walitinga hatua hiyo baada ya kuwaondosha Green Eagles ya Zambia kwa mikwaju ya penalti 4-3 kufuatia kupata sare ya mabao 2-2 ndani ya muda wa nyongeza.Azam FC ambayo ndio bingwa mtetezi wa michuano hiyo inayoandaliwa na Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), inahitaji kutetea taji hilo ililotwaa msimu uliopita baada ya kuifunga Simba mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Iwapo watafanikiwa kulitwaa tena itakuwa ni mara ya tatu.Mara ya kwanza walilitwaa mwaka 2015 kwa kuichapa Gor Mahia ya Kenya mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.KCCA wanaingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya kulikosa taji hilo mwaka 1979 walipocheza fainali dhidi ya Abaluya FC kwa sasa inajulikana kama AFC Leopards ya Kenya baada ya kupoteza kwa bao 1-0.Ushindi dhidi ya Azam FC leo utawafanya kuweka historia nyingine mpya kwao kuchukua taji hilo kwa mara ya pili baada ya kulichukua kwa mara ya kwanza mwaka 1978. | 4 |
GENEVA, USWISI BINGWA wa zamani wa mchezo wa Formula One, Michael Schumacher, hadi sasa inaripotiwa kuwa matibabu yake yamefikia kiasi cha pauni milioni 14 zaidi ya Sh bilioni 36 tangu alipopata ajali Desemba 29, 2013. Nyota huyo wa magari alipata ajali ya gari na kusababisha matatizo ya kichwa ambapo alipoteza fahamu kwa muda mrefu, tangu apate ajali hiyo hadi sasa bado hali yake haijakaa sawa na anaendelea na matibabu huko nyumbani kwake Geneva nchini Uswisi. Matibabu yake kwa kipindi cha miaka mitatu tangu amepatwa na tatizo hilo kwa sasa yamekuwa juu huku bado hali yake imekuwa ya kusuasua japokuwa imekuwa tofauti na miaka miwili iliyopita. Inadaiwa kwamba, nyota huyo wa magari matibabu yake kwa wiki yanafikia kiasi cha pauni 115,000, ambapo ni sawa na 303,582,000 kwa wiki, hivyo kuweza kufikia kiasi cha pauni milioni 13.8, sawa na bilioni 36. Thamani ya nyota huyo wakati yupo katika mashindano miaka mitatu iliyopita ilifikia kiasi cha zaidi ya pauni milioni 500, ambazo ni sawa na zaidi ya Sh bilioni moja. Mke wa nyota huyo, Corinna Betsch, amedai kuwa anaendelea kupambana ili kuhakikisha hali ya mume wake inaendelea kuwa kama awali. Corinna alifanya maamuzi ya kuuza ndege ya mume wake kwa ajili ya kutenga fedha za matibabu, lakini hadi sasa bado hali haijatengemaa. Meneja wa Schumacher, Sabine Kehm, amedai kwa sasa hawana mpango wa kueleza kile ambacho kinaendelea katika hali ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 47. “Tunaendelea kupambana kuhakikisha Schumacher anarudi katika hali yake ya kawaida, lakini si jambo la msingi kuueleza umma hali jinsi inavyoendelea, tutaendelea kulinda kile ambacho tumekipanga. “Habari ambazo zitakuwa zinaenea bila kutoka kwa watu husika zitakuwa hazina ukweli wowote, familia itaweka wazi nini kinaendelea kama itahitajika kuwa hivyo,” alisema Kehm. Meneja huyo aliongeza kwa kuwaomba wadau mbalimbali waendelee kufanya maombi kwa ajili ya nyota huyo aweze kurudi katika hali yake. “Tunathamini mchango wake, tunatambua yale ambayo ameyafanya katika michuano ya Formula One, hivyo ni vizuri kumwombea aweze kurudi katika hali yake ya kawaida, amekuwa mgonjwa kwa muda mrefu sasa ni vizuri kumwombea,” aliongeza. | 4 |
Na FLORENCE SANAWA-MTWARA NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Seleman Jafo, ameagiza watumishi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani waliohusika kutumia zaidi ya Sh milioni 300 za miradi ya ujenzi wa shule na barabara wachukuliwe hatua za kisheria. Kauli hiyo, ameitoa jana wakati wa kikao cha pamoja na watumishi wa Mkoa wa Mtwara na kubaini uwapo wa matumizi mabaya ya fedha za umma. Alisema fedha hizo zilizokuwa zimetengwa kwa ujenzi wa Shule ya Sekondari Umoja, zimeliwa na wajanja. “Hawa watu waliokula fedha za miradi, tuwapeleka mahakamani… haiwezekani fedha zote za wananchi ziliwe kisha watu wapo tu wanaishi, wanahamishwa hapa wanapelekwa sehemu nyingine, wote waliofanya hivi hawatavumiliwa. “Haiwezekani mtu anatafuta mamilioni ya fedha kiasi hiki… hii itakuwa ni ‘network’, tutawatafuta mmoja baada ya mwingine, wa kwanza hadi mwisho, hata kama kuna viongozi wa kisiasa walishiriki tutawachukulia hatua,” alisema Jafo. Alisema fedha za makusanyo ya ndani zilipaswa kutumika kwa maendeleo ya wananchi na kukata asilimia tano ya vijana na wanawake ili wapatiwe mikopo. Jafo alisema aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani, ambaye amehamishiwa Sekretarieti ya Mkoa wa Iringa, Limbakisye Shimwela na aliyekuwa mwekahazina, Christina Buchuma, lazima wachukuliwe hatua. kwa upande wake, Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Beatrice Dominic, alisema baada ya kukuta taarifa ya matumizi ya fedha ambayo haijaainishwa, alichukua uamuzi wa kumpumzisha kazi mwekahazina huyo ili apishe uchunguzi. | 3 |
LEO serikali inatarajiwa kutoa ufafanuzi wa ujenzi wa miundombinu nchini hasa barabara za mikoa na wilaya ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na wabunge kwa kuchelewesha mapinduzi ya kilimo vijijini na kuiweka nchi katika mstari sahihi wa uchumi wa kati.Kwa muda wa siku tatu wabunge wamekuwa wakijadili hoja ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambapo pamoja na kupongeza miradi ya kimkakati walilalamikia ubovu wa barabara hasa zile ambazo zinafanyiwa huduma na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (Tarura).Wabunge waliosimama walitaka Waziri mwenye dhamana, Isack Kamwelwe atakapotoa ufafanuzi leo, kueleza barabara hizo ambazo nyingine ni ahadi za marais wa Tanzania, zitafanyiwa kazi lini huku nyingine zikidaiwa hazipo kwenye hotuba ya bajeti.Wabunge ili kuhimiza ahadi za serikali wanatarajiwa kushikilia kifungu cha mshahara wa waziri kwa mujibu wa kanuni ili kupata maelezo muafaka.Aidha, serikali itajibu ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ambapo pamoja na mambo mengi ilishauri serikali kuacha asilimia 40 ya mapato ya Mamlaka ya Bandari nchini kwa ajili ya kutekeleza miradi yake ya maendeleo.Aidha, kamati hiyo ilishauri kuharakishwa kwa ujenzi wa bandari kavu ili kupunguza gharama za wateja kufika katika bandari ya Dar es Salaam kutoa mizigo.Pia katika masuala ya uchukuzi kamati ya kudumu ilitaka ujenzi wa reli nchini kushirikisha sekta binafsi na mikopo hasa kwa reli ya kusini kutoka Mtwara hadi Mbambabay na Mchuchuma na ile inayotoka Tanga kupitia Arusha hadi Musoma.Aidha reli nyingine ni kutoka Isaka hadi Rusumo. Hoja nyingine zinazotarajiwa kutawala kwa mujibu wa michango ya wabunge ni ujenzi wa reli ya Kati na ile ya SGR, ya Tazara, ATCL na TTCL hasa deni lake la Sh bilioni 28 ambalo lipo katika taasisi mbalimbali nchini.Ikiwa imetengewa bajeti ya miradi ya maendeleo ya Sh trilioni 4.1 sawa na asilimia 34.46 ya bajeti nzima ya miradi ya maendeleo, upande wa upinzani unataka pia maelezo ya serikali ya takwimu za ajira za kudumu au za muda zilizotokana na uwekezaji unaofanyika katika wizara hiyo.“Kambi rasmi ya upinzani inapenda kupatiwa takwimu za ajira za kudumu au za muda zilizotokana na uwekezaji huo... ili watanzania waweze kupima kama fedha za walipa kodi zinaenda kwenye miradi ambayo inaleta matokeo chanya kwa watanzania wote,” alisikika Msemaji Mkuu, Kambi rasmi ya upinzani Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, James Mbatia, Alhamisi iliyopita akiwasilisha hotuba yake.Aidha serikali inatarajiwa kueleza namna inavyotekeleza mpango wa pili wa miaka mitano unaotaka makampuni ya ndani katika kupata kazi za ujenzi kuwa asilimia 60 ya thamani ya jumla ya kazi za ujenzi hapa nchini. Jambo ambalo linaonekana litaleta vuta nikuvute ni shughuli za Wakala wa Majengo (TBA) na hasa miradi inayopatiwa.“Kambi rasmi ya upinzani inapenda kufahamu hiyo miradi inayotoka wizarani na katika idara na taasisi za serikali inaletwa tu kwa TBA kama zawadi au kuna utaratibu wa kufuata sheria ya manunuzi unafanyika,” amehoji Mbatia.Upande wake serikali pia itatoa ufafanuzi kuhusu kuahirishwa kwa ujenzi wa express way ya Chalinze ambayo wabunge walisema hakuna sababu na badala yake atafutwe mzabuni ajenge na watumiaji walipie. | 3 |
MKUU wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel amewakaribisha wananchi wa mkoa huo, mikoa ya jirani na Tanzania kwa ujumla kuhudhuria katika Jukwaa la Fursa za Biashara mkoani Geita linalofanyika kesho.Kiongozi huyo amesema ana hakika litakuwa na manufaa makubwa kwa mkoa wake. Mkuu wa Mkoa amewaeleza waandishi wa habari ofisini kwake kuwa, Jukwaa hilo limetanguliwa na maonesho ya bidhaa za wajasiriamali zinazozalishwa Geita.Amesema maonesho hayo yaliyoanza jana katika viwanja vya Halmashauri ya Mji wa Geita na kwamba yatamalizika kesho sambamba na Jukwaa la Biashara. Alisema Jukwaa litafanyikia katika ukumbi wa Gedeco unaomilikiwa na Halmashauri hiyo ya Mji wa Geita.Gabriel amesema nia kubwa ya kufanyika kwa Jukwaa na maonesho hayo ni kuwasaidia wajasiriamali wa mkoa wake kutangaza fursa walizo nazo sambamba na kukutana na wadau mbalimbali wa maendeleo na hivyo kujifunza kutoka kwao ili kuweza kupanuka zaidi kibiashara."Wajasiriamali watakapokutana na wadau mbalimbali wa biashara kwenye jukwaa kesho, watakuwa wanaongea lugha moja ya biashara na uwekezaji ili kunyanyua mkoa wa Geita," alisema.Alisema katika jukwaa hilo, ana hakika wajasiriamali wa Geita watapata ujuzi, elimu na hata masoko kwa ajili ya kuboresha shughuli zao."Wajasiriamali wetu watakutana na taasisi za fedha na kujua ni taasisi ipi inaweza kuwasadia kukuza mitaji yao," alisema.Alisema jukwaa hilo pia linausaidia mkoa kutangaza fursa zake kwa Watanzania, fursa ambazo zimekuwa pia zikiandikwa na vyombo mbalimbali vya habari, hususani vya Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN).Mkuu wa mkoa ameishukuru TSN kwa kuanzisha majukwaa ya biashara na kuwa tayari kushirikiana na ofisi yake ili kufanikisha Jukwaa la Biashara la kesho.Kaimu Mhariri Mtendaji wa TSN, Tuma Abdallah, amesema ana matarajio makubwa kwamba Jukwaa la Biashara la kesho litakuwa na msisimko wa aina yake kutokana na maandalizi yaliyofanyika na hasa ushirikiano mkubwa uliotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita.Akielezea kwa nini TSN imeamua kufanya majukwaa ambapo hili ya Geita ni la saba, Tuma amesema ni kutokana na kuona kwamba taasisi hiyo ya serikali ina dhima ya kusaidia na kuleta chachu katika kuboresha biashara na uwekezaji kwa maendeleo ya taifa.Amesema, lengo la majukwaa hayo ni kuibua fursa za biashara na uwekezaji katika maeneo husika.Alisema timu ya TSN imekaa mkoani Geita kwa karibu wiki tatu, imetembea maeneo mbalimbali ya mkoa na kuzungumza na wadau mbalimbali kuhusu maendeleo ya mkoa wa Geita na kisha kusambaza habari za maeneo hayo na kwamba kesho kutakuwa na toleo maalumu la mkoa wa Geita kwenye gazeti hili.Tayari kampuni kadhaa zimejitokeza kudhamini Jukwaa la Geita ikiwa Geita Gold Mine (GGM), Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Maelezo Televisheni, TADB Bank, Benki ya NBC na Busolwa Mining Limited.Wadhamini wengine ni Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko Hifadhi ya Jamii (SSRA), Benki ya Azania, Lenny Hotel, Waja General Company Ltd, GF Truck, Air Tanzania Corporation Ltd, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA).Zikiwa zimebaki saa chache Jukwaa kufanyika, wadhamini wanakaribishwa kupitia namba zifuatazo: 0655 332 866, 0712 516 169 au email: advertising@dailynews.co.tz | 5 |
MABISHANO makali ya kisheria na ulinzi usio wa kawaida wa askari Polisi ni miongoni mwa mambo yaliyojitokeza siku ya kwanza ya usikilizwaji wa rufaa ya kufutiwa dhamana kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko.Katika mabishano ya jana, upande wa mashitaka ulipinga hoja za rufaa ya Mbowe na Matiko na kuiomba mahakama itupilie mbali rufaa hiyo.Mahakama hiyo leo itatoa uamuzi wa ama kutengua maamuzi ya Mahakama ya Kisutu au kukubaliana na maamuzi yaliyotolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri. Mawakili wa serikali, Faraja Nchimbi, Simon Wankyo na Dk Zainabu Mango walipinga rufaa hiyo kwa hoja tatu kwa Jaji Sam Rumanyika wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.Rufaa hiyo ilisikilizwa kwa dakika 150, kuanzia 2:30 hadi saa 5 asubuhi, huku kukiwa na ulinzi mkali wa askari Polisi zaidi ya 19 wenye silaha za moto na mabomu ya machozi ili kuhakikisha usalama unakuwepo muda wote mahakamani.Katika hatua nyingine, Mbowe na Matiko waliwasili katika Mahakama hiyo wakiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza wanane. Ukiwasilisha pingamizi za rufaa hiyo, upande wa mashitaka uliiomba mahakama hiyo itupilie mbali rufaa hiyo kwa sababu tatu walizodai.Walitaja sababu ya kwanza kuwa ni warufani kushindwa kukata rufaa kupinga dhamana iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu hivyo haina mamlaka ya kusikiliza rufaa kwani taarifa ya kusudio la kukata rufaa haipo.Wakili Nchimbi alidai hoja kuwa masharti ya dhamana waliyopewa washitakiwa si sahihi kisheria kwa sababu Mahakama ya Kisutu ilitoa masharti ya dhamana kwa mwongozo wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).Alidai tangu mahakama ilipotoa masharti ya dhamana kati ya Machi na Aprili, mwaka huu, hayajawahi kukatiwa rufaa na warufani, kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa wala kuomba kuongezewa muda kukata rufaa.“Hatujawahi kupokea maombi ya aina yoyote kupinga masharti ya dhamana dhidi ya wakata rufaa. Hii inaonesha waliridhika na masharti yote.“Hoja masharti waliyopewa washitakiwa yako kinyume na sheria si sahihi, kwani wana mawakili madhubuti ambao wangeweza kuliona suala hilo mapema,” alidai Nchimbi.Pia alidai mahakama inapaswa kujikita katika haki ya msingi ya pande zote kwani Ibara ya 13 (6) (a) inawapa haki kusikilizwa na isipofanya hivyo watanyimwa haki ya msingi ya kikatiba.Alidai kitendo chao cha kuomba mahakama iwapatie muda wa kusoma na kujibu rufaa hiyo hakikuwa na lengo la kuchelewesha kesi na haina maana ya kuvunja haki kwani endapo kuna uharaka, ufanyike lakini haki zifuatwe.Wakili wa Serikali Mkuu, Dk Zainabu Mango alidai taarifa ya kusudio la kukata rufaa iliyowasilishwa na wakata rufani si sahihi.Alidai kifungu cha sheria kilichotumika katika taarifa ya kusudio la kukata rufaa hakiipi mahakama mamlaka ya kusikiliza rufaa hiyo kwani si sahihi, hivyo inapaswa kutupwa mbali.“Sheria inaelekeza rufaa inayoletwa inatakiwa kutoa notisi ya siku 10 lakini haijafanyika hivyo na kifungu kilichotumika hakiipi mahakama mamlaka ya kusikiliza rufaa,” alidai Dk Mango.Wakili Wankyo kwa upande wake, alidai rufaa hiyo haijakidhi matakwa ya sheria kifungu cha 362 (1) kuhusu mwenendo wa shauri kuambatanishwa katika rufaa iliyokatwa.Alidai tangu kesi ya msingi ifunguliwe, kuna mambo mengi yaliyotokea ambayo mahakama ingeyapata yangesaidia kuiongoza kutenda haki.“Nyaraka za mwenendo wa shauri tuliopatiwa zina upungufu kwani hazisomeki vizuri kwani kuna baadhi ya maneno yamekatwa na ilitakiwa tuzipate mara baada ya kuwasilisha rufaa hii ili tufanye maandalizi ya kutosha kwani tunaamini yapo mambo mengi yalizosababisha kufutwa kwa dhamana kwa warufani,” alidai Wankyo.Akijibu hoja hizo, Wakili wa Utetezi, Peter Kibatala kwa niaba ya warufani alidai sababu za upande wa mashitaka hazina mashiko kisheria kwani iko kimya kuhusu kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa kwamba inawezekana wakatoa kwa taarifa ya mdomo au maandishi.Alidai anayekata rufaa kutoka Mahakama ya Wilaya kwenda Mahakama Kuu inaelekeza taarifa ifanyike hata kwa mdomo lakini rufaa kutoka Mahakama Kuu kwenda Mahakama ya Rufani inatakiwa iwe ya maandishi.Alidai walitoa taarifa ya kusudio la kukata rufaa kwa mdomo mara Mahakama hiyo ilipotoa uamuzi wake Novemba 23, mwaka huu.Kuhusu mwenendo wa shauri, Kibatala alidai walikubaliana kutumia mwenendo wa shauri la Mahakama ya Kisutu ilivyoelekezwa na ni kweli mwenendo huo umekosewa lakini walipaswa kuendelea kuusoma ili kuelewa.“Mwenendo huu wa shauri si mgeni kwao kwa sababu wao ndio walioandaa hati ya kiapo cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni na Ofisa wa Idara ya Uhamiaji.“Sisi tumetaka mwenendo wa shauri kuanzia Novemba Mosi hadi Novemba 23, mwaka huu na tangu mwanzo wa kesi hii,” alidai Kibatala.Hata hivyo, Jaji Rumanyika alimhoji Kibatala endapo mahakama hiyo itatengua maamuzi ya Mahakama ya Kisutu, masharti ya kuwataka washitakiwa kuripoti polisi si yatabaki yalivyo? Alidai mahakama itaamua ifanye nini kwani wanajiandaa kulalamikia uamuzi wa awali.Jaji Rumanyika pia alihoji kama Mahakama ya Kisutu inaweza kubadilisha uamuzi, si ingeacha bila kuleta hoja ya masharti ya dhamana na kuhoji kama warufani walikuwa na mpango wa kukata rufaa dhidi ya masharti yaliyotolewa.Mahakama hiyo leo itatoa uamuzi wa ama kutengua maamuzi ya Mahakama ya Kisutu au kukubaliana na maamuzi yaliyotolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.Katika rufaa yao washitakiwa hao kwa kupitia Wakili Kibatala walidai wana sababu nne za kupinga uamuzi wa Mahakama ya Kisutu ikiwemo Mahakama hiyo kutowapa nafasi ya kujieleza wadhamini kwa mujibu wa sheria.Pia alidai mahakama imekosea kuwafutia dhamana washitakiwa kwa sababu Novemba 12, mwaka huu Mbowe na Matiko walifika mahakamani bila kukamatwa na bila kuwa chini ya ulinzi.Alidai masharti ya dhamana waliyopewa washitakiwa ni kinyume na sheria. | 3 |
MANCHESTER, ENGLAND BAADA ya klabu ya Manchester City kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England, Chelsea, kocha wa timu hiyo, Pep Guardiola, amefunguka na kusema hana mpinzani kutokana na ubora wa kikosi chake. Kocha huyo anaamini kuwa kikosi chake kinaweza kwenda kucheza nje ya Uwanja wa Etihad na kufanikiwa kupata matokeo mazuri, hivyo anaamini hakuna mpinzani ambaye anaweza kumtisha kwa sasa. Man City juzi walikuwa kwenye Uwanja wa Stamford Bridge na kiungo wake, De Bruyne, alikuwa mchezaji wa pekee ambaye aliwafanya mashabiki wa Chelsea walale na viatu baada ya kichapo hicho. “Jambo muhimu kwetu lilikuwa kushinda kwenye Uwanja wa Stamford Bridge na kuondoka na pointi tatu, nataka kuifanya Manchester City kuwa kwenye ubora wa hali ya juu kwenye michuano ya Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa Ulaya. “Kwa sasa ninaamini wachezaji wapo pamoja na mimi kutokana na kufuata yale ninayowaelekeza, kila mmoja alikuwa anajua ubora wa Chelsea, lakini tuliweza kuushambuliaji Uwanja wa Stamford Bridge kuanzia dakika ya kwanza hadi tunapata ushindi, hicho ndicho nilichokuwa nataka kukifanya kwa klabu hii. “Msimu uliopita nilikuja kwenye uwanja huo lakini matokeo hayakuwa mazuri kwangu, lakini safari hii kutokana na ubora wetu tumefanikiwa, nakumbuka nimepoteza michezo miwili yote msimu uliopita, lakini msimu huu sipo tayari kupoteza,” alisema Gaurdiola. Hata hivyo, kocha huyo ameweka wazi kuwa alichobakisha ni kucheza na timu mbili ambazo kwake ni ngumu, Tottenham na wapinzani wake Manchester United. “Najua nina kibarua kizito siku ambayo nitakutana na kocha Jose Mourinho na kikosi chake cha Manchester United, najua uwezo wake, najua uwezo wa wachezaji wake, wanakuwa na matokeo mazuri kila siku, wana kasi kubwa na wanaweza kupiga mipira mirefu. “Ugumu mwingine ni kukutana na Tottenham ambayo ina mshambuliaji wake, Harry Kane, lakini nitahakikisha ninashinda michezo yote dhidi yao bila ya wasiwasi,” aliongeza. Msimu uliopita klabu ya Chelsea ilimaliza Septemba bila ya kupoteza hata mchezo mmoja, lakini msimu huu wamejikuta wakishindwa kuipiku rekodi hiyo baada ya kichapo hicho mbele ya mashabiki wake. Michezo mingine ya juzi ni pamoja na West Ham ikitoka na ushindi wa bao 1-0, West Brom ikitoka sare ya 2-2, Stoke City ikishinda mabao 2-1 na Leicester City ikitoka suluhu.
| 4 |
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo ifi kapo Juni 30, mwaka huu, wawe wamekamilisha ununuzi wa mashine za kielektroniki za kukusanyia mapato.Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), Dk Mahenge alisema halmashauri zote saba zinatakiwa kukamilisha ununuaji wa mashine za kukusanyia mapato (POS) na akazipongeza ambazo tayari zimekamilisha ununuzi huo.Amemuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Muduka Kessy kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha halmashauri za Kondoa Mjini, Vijijini, Chemba, Bahi, Jiji, Kongwa, Chamwino na Mpwapwa zinakamilisha ununuzi wa mashine hizo.Dk Mahenge ameipongeza Halmashauri ya Kondoa Vijijini ambayo imenunua mashine 59 na hivyo hakuna kituo cha kukusanya mapato ambacho hakina mashine hiyo.Ameipongeza pia halmashauri ya Kondoa Mjini kwa kuweka lengo la kununua mashine 56 na kuvuka lengo kwa kuongeza mashine tatu zaidi kwa ajili ya kukusanya mapato.Akaziomba zote zilizobaki kuhakikisha kwamba zinakamilisha ununuzi huo, ambapo takwimu zinaonesha kwamba Halmashauri ya Kongwa haijakamilisha mashine 77, kati ya 150 zinazotakiwa, hivyo inatakiwa kutumia fedha za ndani au kukopa ili kupata mashine hizo.Pia takwimu zinaonesha kwamba, Halmashauri ya Chemba bado mashine 65, kati ya mahitaji ya mashine 130, hivyo mikakati madhubuti inahitajika ili kununua mashine zilizobaki.Halmashauri ya Bahi bado mashine 20, kati ya 80 zinazotakiwa kuwapo katika maeneo mbalimbali ya kukusanya mapato katika wilaya hiyo na kuachana na mtindo wa kutumia risiti.Pia aliitaka, Halmashauri ya Chamwino ambayo bado mashine 50, kati ya 120 zinazotakiwa kuwapo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, kuhakikisha nayo inakamilisha.“Halmashauri ya Mpwapwa imenunua mashine 110 kati ya mashine 113 na hivyo bado mashine tatu, hivyo inatakiwa kukamilisha idadi ya mahitaji yake kupitia mkakati wa kukamilisha katika robo ya nne ya mwaka (Aprili-Juni),” alisema.Akisoma takwimu katika halmashauri ya Jiji, mkurugenzi wake, Godwin Kunambi alisema ina mashine 339 za kukusanyia mapato ambazo ni zaidi ya malengo ya mashine 336.Alisema mashine zilizoongezeka zimewekwa katika maeneo yaliyobuniwa ya makusanyo ya mapato na mkakati ni kupeleka katika shule ili kuhakikisha kila mapato yanayoingia yanaingizwa kwenye mashine hizo.Alizitaka halmashauri nyingine zilizobaki kuhakikisha zinakamilisha ifikapo Juni 30, mwaka huu, ambao ni mwisho kutokuwa na mashine hiyo, ili kuondoa mwanya wa kupotea mapato ya mkoa.Mkuu wa Mkoa, Dk Mahenge aliwataka viongozi wa halmashauri hasa wakurugenzi kuhakikisha wanatekeleza maazimio yanayofikiwa katika vikao, kwani tayari jambo la kila halmashauri kuwa na mashine hizo lilijadiliwa na kuwekewa maazimio katika vikao vilivyotangulia. | 5 |
Karibu miezi miwili iliyopita klabu hiyo ilitangaza zabuni kwa wanachama wenye uwezo na mtaji kuanzia Sh bilioni 20 kujitokeza na kufanya uwekezaji katika klabu hiyo iliyopania kubadilisha muundo wa uendeshaji kuwa wa hisa.Akizungumza jana Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara alisema mkutano huo utafanyika kuanzia asubuhi kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere. Alisema anaamini huo utakuwa ni mkutano wa kihistoria kwa sababu wanakwenda kubadilisha muundo.“Tunapokwenda kubadilisha mfumo wa uendeshaji tunategemea klabu yetu itakuwa ni tajiri na kuwekeza kwenye miundombinu, itakuwa ina uwezo wa kununua wachezaji bora watakaowezesha kuwa na ligi bora Tanzania na kushinda mataji mengi klabu bingwa Afrika,”alisema.Awali, klabu hiyo ilisema mwekezaji atamiliki asilimia 50 ya hisa huku asilimia 10 zikitarajia kugawiwa kwa wanachama hai na nyingine 40 kuuzwa kwa wanachama. Tayari mfanyabiashara na mfadhili wa Simba, Mohamed Dewji aliwahi kuonesha nia ya kuwekeza iwapo tu atapewa asilimia 50 ya hisa, ingawa hata hivyo, kesho itajulikana kama atakuwa yeye au wengine kutokana na vigezo vilivyokuwa vimewekwa.Hata hivyo, kazi bado ipo kwa Simba kwani Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limefanya marekebisho ya kanuni zake na juzi kutoa waraka kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) unaotoa maelekezo ya ununuaji na uuzwaji wa hisa za klabu au Chama cha Michezo.Marekebisho yaliyopo ni kwamba vyama au klabu zilizoanzishwa na wanachama vikiamua kuuza hisa zake vinapaswa kutenga asilimia 51 kwa ajili ya wanachama na asilimia 49 kwa wanaotaka kununua.Pia, wanatakiwa kupitia kwenye mamlaka ya mitaji na masoko ili kuidhinishwa na baadaye kurudi kwenye soko la hisa ili kufuata taratibu za uuzwaji na ununuaji. Manara alisema tayari wamepata taarifa hiyo kutoka TFF na wanaendelea na mazungumzo na Dk Mwakyembe kuhusu taratibu hizo mpya na namna ya kubadili kanuni wakati wakiendelea na mchakato wao wa kutangaza mwekezaji. | 4 |
RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kutowachagua wagombea uongozi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, utakaofanyika baadaye mwaka huu na Uchaguzi Mkuu wa mwakani watakaotoa rushwa.Aliyasema hayo mjini Geita jana alipokuwa akizindua nyumba 20 za makazi ya askari polisi katika eneo la Magogo mjini Geita. Rais Magufuli alisema wakati uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unakaribia ni vizuri kwa wananchi kuanza kutafakari juu ya viongozi wazuri watakaowasaidia kuwaletea maendeleo na si kuwachagua kwa rushwa.“Mkachague viongozi waadilifu, mchague viongozi ambao watakuwa ni watumishi wa wananchi na hasa wanyonge. Msichague wala rushwa, wakiwapa hela zao chukueni, kuleni lakini kura msiwape,” alisema Rais Magufuli. Alisema viongozi wakipatikana kwa njia ya rushwa, watakuwa wanasimamia miradi yenye maslahi yao binafsi badala ya kusimamia maendeleo yenye maslahi mapana kwa wananchi wanyonge wa Tanzania.Alisema ili kufanikisha uchaguzi wa serikali za mitaa, Jeshi la Polisi lina wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa linaendelea kutunza amani na utulivu, ili uchaguzi huo uweze kufanyika vizuri na kuwezesha kupatikana kwa viongozi wazuri.Kuhusu makazi ya askari, Rais Magufuli alisema serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha makazi na utendaji kazi wa askari ili jeshi hilo liweze kufanya kazi ya kusimamia amani na utulivu wa nchi lakini pia maisha na mali za wananchi.Alisema pamoja na kazi kubwa inayofanywa na jeshi hilo lakini wapo wanasiasa ambao wanatoa maneno ambayo yanavidhalilisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa maslahi yao na aliwataka kuacha kufanya hivyo na badala yake kuwatia moyo askari ili waendelee kufanya kazi zao kwa bidii na weledi mkubwa.Hata hivyo, alisema wapo askari ambao wamekuwa wanakiuka maadili ya kazi yao na alimwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro kuendelea kuwafukuza kazi askari wote watakaobainika kukiuka misingi na maadili ya kazi yao na kulipaka matope jeshi hilo. | 3 |
BINGWA mtetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara, Simba leo wanashuka dimbani kuikabili timu ya Ligi Daraja la Kwanza ya Arusha FC, katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) utakaochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Mchezo huo ni mtihani wa kwanza kwa benchi jipya la ufundi likiongozwa na Kocha Mkuu Sven Vanderbroeck na msaidizi wake Selemani Matola waliojiunga na timu hiyo baada ya waliokuwepo kufungishwa virago.Wekundu hao huenda wakawa makini msimu huu, kuhakikisha wanaheshimu wapinzani wao licha ya udogo ili yasije kuwarudia ya misimu miwili iliyopita. Msimu uliopita wekundu hao walitolewa na timu ya Daraja la kwanza ya Mashujaa raundi ya tatu ya michuano hiyo kwa kipigo cha mabao 3-2 na msimu wa 2018 walitolewa na Green Warriors kwa sare ya 1-1 na kutolewa kwa penalti 4-3.Timu hizo zinakutana zikiwa na viwango tofauti, Simba ndiye kinara wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 25, ikijivunia kucheza michezo 10, ikipoteza mmoja, sare moja na kushinda nane. Safu yake ya ushambuliaji inayoongozwa na Meddie Kagere na Miraji Athuman imekuwa ni hatari zaidi inapokuwa karibu na lango la wapinzani hivyo, Arusha isipokuwa makini huenda ikachezea mvua ya mabao.Pia safu ya ulinzi sio mbaya kwani imeruhusu mabao matatu kwenye nyavu zake katika michezo 10 waliyocheza. Arusha FC pia, sio timu mbaya, ipo kundi B Ligi Daraja la Kwanza ikishika nafasi ya nne kwa pointi 16 baada ya kucheza michezo 10. Ushindi wao utategemea namna walivyojiandaa kimbinu kila mmoja ukizingatia mechi ni za mtoano. | 4 |
IKIWA zimebaki siku tatu, kuanza kwa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki, Jiji la Dar es Salaam limeweka mikakati mbalimbali kwa ajili ya kutekeleza agizo hilo katika mitaa mbalimbali.Aidha, uongozi wa mkoa, umeahidi kuwa kazi ya kutokomeza mifuko hiyo, haitakuwa ya nguvu wala usumbufu wowote na tayari vikosi kazi vimeshaundwa.Akizungumza jijini Dar es Salaam, katika mkutano wa viongozi mbalimbali wa jiji hilo, Katibu Tawala wa Mkoa, Abubakar Kunenge amesema mkakati huo una maeneo manne yakilenga katika kusimamia sheria na kanuni ambazo zitasaidia katika kutokomezwa kwa mifuko hiyo ambayo ina madhara makubwa.Alisema katika kutekeleza mkakati huo, elimu kwa umma ni jambo litakalozingatiwa, usimamizi na uratibu, eneo ambalo mifuko hiyo itawekwa pamoja na usimamizi na pamoja na kufanya kazi na wadau mbalimbali.“Dar es Salaam inaendelea kutoa taarifa ya maelekezo kwa wananchi, pia tunaendelea kutayarisha mabango ambapo mpaka sasa yameshatayarishwa saba pamoja na manispaa mbalimbali,” alisema Kunenge na kuongeza kuwa magari yanaendelea kupita mitaani kuelimisha wananchi.Alisema elimu ni suala endelevu kwa wananchi na kwa kiwango kikubwa wameonesha utayari wa kuacha matumizi ya mifuko hiyo, hivyo agizo hilo ambalo lilitolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa litafanikiwa kwa kiwango kikubwa.Alisema katika eneo la usimamizi tayari vikosi kazi mbalimbali vimeundwa kwa ajili ya kuwajibika na kuripoti kuhusu suala zima la utekelezwaji wa udhibiti wa mifuko hiyo na wakuu wa wilaya watapita katika maeneo yao kuona yaliyopangwa na utekelezaji wake.“Wananchi wameelezwa mahali pa kuweka mifuko hiyo, kuna vituo mbalimbali vya kukusanya vipatavyo 137 na katika vituo hivyo, mifuko haitakiwi kukaa kwa muda mrefu,” alisema Kunenge na kufafanua kuwa katika vituo hivyo vitakuwa vimefungwa kuepuka upepo lakini pia kutakuwa na walinzi kuepusha wananchi kufika na kuchukua mifuko tena.Alisema katika maeneo mbalimbali watu wameshatenga maeneo kuanzia ngazi ya mtaa kwa ajili ya kukusanya mifuko hiyo na kwamba kazi ya kuondoa mifuko pamoja na kupiga faini haitegemewi kuwa ni chanzo cha ufisadi na taarifa zitatolewa mara kwa mara.Awali Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema kazi ya kuzuia matumizi ya mifuko hiyo haitakuwa ya kutumia nguvu wala usumbufu wowote.“Jiji hili ndilo linalozalisha na kutumia mifuko hiyo kwa kiwango kikubwa, tukiweza kupiga hatua kwa asilimia 60 itakuwa ni hatua kubwa imefanyika,” alisema. | 3 |
WATOTO 67 wa kike kati ya 2,572 waliokimbilia Kituo cha Msanga kinachopokea na kulea watoto wa kike waliokimbia nyumbani kwao kuogopa kukeketwa, wamekataliwa na wazazi pamoja na walezi wao. Kutokana na kitendo hicho, kituo hicho kimechukua jukumu la kuwapeleka shule kuanza masomo kwa mwaka huu, huku kikiiomba Serikali kuingilia kati kwa kuwachukulia hatua wazazi na walezi waliokataa kuwapokea watoto hao. Akizungumza wakati wa kufunga mahafali ya kufunga kambi, Meneja wa mradi wa Association For Termination of Female Genital Multilation (ATFGM) ulio chini ya kituo hicho, Valerian Mgani, alisema wamesikitishwa na wazazi na walezi kukataa kuwapokea watoto hao. Alisema wazazi hao wamewakataa watoto hao kwa sababu walikimbia makazi yao kukwepa kutii mila zao. “Kama wazazi, walezi na jamii imewakataa watoto hawa sasa tunafanyaje, kituo kimebeba jukumu la kuwapeleka shuleni kusoma, ikiwamo shule za msingi na sekondari. “Tangu kuanzishwa kwa kituo hiki mwaka 2008, tumekuwa tukipokea watoto ambao wanakimbia ukatili, ikiwemo ukeketaji na wengine kwa ajili ya kupata elimu juu ya tohara mbadala kutoka wilaya za Serengeti, Tarime, Loliondo na nchi jirani ya Kenya. “Huwa kuna utaratibu wa mafunzo ya muda katika kambi zetu, tunatenga baadhi ya watoto na kuwapa elimu kwa kuwahusisha wazazi, na kambi zinapomalizika watoto hao hulazimika kurudishwa nyumbani kwao, lakini baadhi yao wamekataliwa na wazazi wao kwa kile kinachodaiwa kuwa wamekataa mila kwa kukimbia kukeketwa… hadi sasa kuna mabinti 67 waliokataliwa,” alisema. | 3 |
NAHODHA na mchezaji mkongwe kwenye kikosi cha Yanga Kelvin Yondani, ameelezea kufurahishwa na mwenendo wa timu hiyo tangu kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.Kabla ya mechi za leo Yanga inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 22 na imecheza michezo minane ikiwa ni pungufu dhidi ya vinara wa ligi hiyo Azam FC wenye pointi 24 na mabingwa watetezi Simba ambao wapo nafasi ya tatu na pointi zao 20. Simba na Azam zinacheza leo. Yondani amesema imani yake ni kuona jeshi lake linaendelea kupambana na kuhakikisha wanaisaidia Yanga inafikia malengo iliyojiwekea na hilo linawezekana kutokana na ari waliyokuwa nayo na kwamba mashabiki na wanachama wao watafurahi.“Tumecheza mechi nane na kitu kizuri hatujapoteza tupo nafasi ya pili jambo zuri ni kuona wachezaji bado wana ari kubwa ya kupambana na kuipigania timu yao kupata matokeo mazuri,” alisema Yondani.Nahodha huyo mwenye mchango mkubwa kwenye kikosi cha mabingwa hao wa kihistoria alisema kadri ligi inavyoendelea kushika kasi ndiyo wanazidi kuimarika hivyo hadhani kama mwendo walioanza nao unaweza kupungua kama ambavyo watu wanafikiria.Alisema lipo kundi kubwa la watu wanaponda ushindi wanaoupata kutokana na mechi zote kucheza nyumbani lakini kwake haoni kama kuna ukweli kutokana na namna walivyojipanga msimu huu.“Baadhi ya watu wanaponda ushindi wetu kutokana na mechi zote kucheza nyumbani lakini ukiangalia mechi zote tulizoshinda tumepambana kwa jasho letu wenyewe na tumeshinda kwa haki hivyo wanaosema hivyo ni chuki zao dhidi yetu,” alisema Yondani.Kocha mkuu wa timu hiyo Mkongomani Mwinyi Zahera, alisema kuna uwezekano mkubwa wa lengo walilojiwekea kufanikiwa mwishoni mwa msimu huu kutokana na wachezaji wake kufuata vyema mbinu anazowapa.Alisema kikosi kucheza mechi nyingi nyumbani kwenye uwanja wa taifa kumewasaidia kuimarisha kiwango chao na kuwajengea wachezaji wake ari ya kujiamini ndiyo maana wamekuwa wakipata ushindi wa mfululizo.“Hatukuwa na maandalizi mazuri kujiandaa na msimu lakini nafurahi kuona kila siku tunazidi kuimarika na kuwa bora naamini usajili tulioufanya umeonyesha thamani yake ingawa ndiyo mwanzo na bado mapungufu tunayo lakini mazuri yanakuja,” alisema Zahera.Kocha huyo alisema uwepo wa wachezaji wakongwe kama Yondani na Thabani Kamusoko na Amissi Tambwe kumeifanya timu hiyo kuwa na uwiano mzuri ndani ya uwanja ndiyo maana wamekuwa wakicheza kwa uelewano mzuri.Alisema baada ya dirisha dogo amepanga kuongeza wachezaji wachache ili kuzidi kukiimarisha vyema kikosi chake kwa ajili ya kumalizia ngwe iliyobaki na kuhakikisha wanafikia malengo yao.Yanga keshokutwa inatarajia kushuka kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam, kuwakabili Lipuli FC mchezo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani wa aina yake kutokana na ubora wa timu hiyo kutoka Iringa. | 4 |
VYUO vikuu vya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), vimefanya vizuri katika masuala mbalimbali ikiwemo taaluma, ikilinganishwa na vyuo vikuu vingine katika Bara la Afrika.Hayo yamebainishwa katika utafiti, uliotolewa wiki iliyopita na Mtandao wa Kulinganishwa Vyuo Vikuu Duniani (Webometrics Ranking).Kwa mujibu wa mtandao huo, Afrika Mashariki imebebwa na vyuo vikuu vinne.Mtandao huo umeonesha kuwa Chuo Kikuu cha Nairobi kimeongoza katika EAC na kimeshika nafasi ya 10 kati ya vyuo 1,686 vilivyoko katika Bara la Afrika.Chuo Kikuu cha Makerere cha Uganda kimeshika nafasi ya pili kwa ubora katika vyuo vya Jumuiya ya Afrika Mashariki na kimeshika nafasi ya 14 kati ya vyuo 1,686 barani Afrika.Chuo hicho kikongwe katika Afrika Mashariki, kimeporomoka kwa nafasi nane, kwa kuwa mwaka jana kiliorodheshwa kama chuo bora cha sita barani Afrika, kikitanguliwa na vyuo vya Afrika Kusini.Pia kilikuwa ndicho chuo bora Afrika Mashariki.Mtandao huo umekiweka Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya, kuwa ni chuo cha tatu kwa ubora katika vyuo vya Afrika Mashariki na cha 23 kwa ubora, kati ya vyuo 1,686 vilivyoko Bara la Afrika. | 3 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.