name stringclasses 429 values | text stringlengths 0 767k ⌀ |
|---|---|
Msimu wa kilimo wa mwaka 2022, Tanzania ilizalisha tani 5,152 za soya, kutoka tani 44,106 zilizozali | Msimu wa kilimo wa mwaka 2022, Tanzania ilizalisha tani 5,152 za soya, kutoka tani 44,106 zilizozalishwa mwaka 2021.
Anguko hilo la uzalishaji wa soya ni mara nane zaidi ya kiasi kile kilichozalishwa katika mwaka 2021, kwa mujibu wa taarifa ya hali ya uchumi ya mwaka 2022.
Ingawa taarifa hiyo inaweka wazi kuwa, mabadiliko ya tabianchi ndiyo mzizi wa tatizo, gharama kubwa za uzalishaji zinazozidi faida inayopatikana ndiyo kiini cha anguko hilo, kwa mujibu wa wakulima.
Licha ya juhudi zinazofanywa na Serikali kuhamasisha kilimo cha Soya, kuna matumaini duni ya wakulima kuendelea kujihusisha na kilimo hicho, kama inavyofafanuliwa na Sada Mponzi, mkulima wa Soya, katika Kata ya Uhambingeti mkoani Iringa.
“Nimeacha kulima mwaka huu, nilikuwa nalima tunauza kwa kilo na kila kilo moja ni Sh1,000 hadi Sh1,300 ni fedha ndogo isiyolingana na gharama za uzalishaji,” alisema.
Akizungumza na Mwananchi, Sada alisema si yeye pekee wengi katika Mkoa huo wameacha kulima zao hilo na kugeukia, alizeti na ufuta kwa kuwa bei yake inaeleweka.
Kulingana na mkulima huyo, wakati biashara hiyo inafanywa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani, waliambia wataongezewa fedha iwapo bei itaongezeka, lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika.
“Ni hasara tu, wateja wenyewe hakuna, unalima hujui unauza wapi, watu wengi wameamua kulima mazao mengine ambayo wanakuwa na uhakika wa kuuza,” alieleza.
Hata hivyo, aliweka wazi kuwa kilimo cha soya kinahitaji gharama lukuki kwa kuwa zao hilo, huoteshwa kwa mbolea, hukua kwa dawa na kupaliliwa mara kadhaa.
“Kila unachofanya ni fedha kuanzia kuandaa shamba hadi unavuna ni fedha nyingi, unakuja kuuza kilo moja Sh1,000 sio sawa, wengi tumekata tamaa.
“Wewe fikiria wakulima walikaa na mazao shambani muda mrefu walipovuna wakakaa nayo ndani bila kupata mteja tumeshakata tamaa,” alisema.
Mbadala wa kilimo hicho, Sada alisema wamegeukia kilimo cha mahindi na alizeti.
Kinachoelezwa na Sada hakitofautiani na Selemani Kibinda anayefanya shughuli hiyo katika Kijiji cha Peapea, wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro.
“Shida kubwa hakuna soko la uhakika, soko lake lina tofauti na mazao yote ambayo wananchi wanajituma kwa hiari kuyalima,” alisema.
Kwa sababu gharama za uzalishaji ni kubwa, alisema wakulima walitarajia kungekuwa na soko la uhakika, lakini kwa hali ilivyo wanahamia katika mazao mengine.
“Zao hili linaathiriwa sana na wadudu, magonjwa mbalimbali kama ukungu na wakati wa kupanda ni aina moja tu ya mbolea ndiyo itakuhakikishia kuota kwake, sasa kwa mambo haya afadhali kungekuwa na uhakika wa soko,” alisema.
Ingawa Serikali inazungumza kuhusu uwepo wa masoko ya kimataifa, Kibinda alisema hakuwahi kupata taarifa hiyo wala hafahamu namna ya kuyafikia.
Katika shamba la nusu ekari, Kibinda alisema ana uhakika wa kuzalisha gunia 1.5 na faida yake itatokana na bei ya sokoni.
Wengi kati ya wanaonedelea na uzalishaji wa zao hilo, ni wale ambao wenyewe pia huchakata kutengeneza unga, maziwa, majani ya chai na bidhaa nyingine kama anavyoeleza Angelika Kitime,mkulima wa soya Iringa.
“Mimi nalima kinachonifanya niendelee ni kwa sababu nachakata kutengeneza bidhaa mbalimbali, lakini kwa Iringa yote hii mashine ya kuchakata ipo moja pekee, kwa hiyo wengi wanashindwa,” alisema.
Alisisitiza tija ya uzalishaji wa zao hilo, itapatikana iwapo mkulima ataamua mwenyewe kuchakata na kuzalisha bidhaa nyingine, jambo ambalo linagharimu. |
Umekutana na nini kilichokuonyesha tofauti ya ulichofunzwa na uhalisia wa maisha ya sasa? Au mwenzet | Umekutana na nini kilichokuonyesha tofauti ya ulichofunzwa na uhalisia wa maisha ya sasa? Au mwenzetu mafunzo uliyopewa yanaakisi unayokutana nayo?
Maswali hayo yanajenga msingi wa hoja ya kukithiri kwa mabadiliko ya mwenendo wa maisha, unaohitaji mfumo na mbinu mpya ili kuishi katika ulimwengu wa sasa.
Unakumbuka ulifundishwa kila unapokutana na aliyekuzidi umri unapaswa kumsalimia kwa kusema shikamoo? Lakini sasa neno hilo baadhi hulitafsiri kama uchoyo na badala ya marahaba majibu yake ni ‘unataka kuninyima nini.’
Sijasahau mafunzo ya wahenga kwamba, napaswa ama kumuachia kiti au kumpokea mwanamke mwenye mtoto anapopanda kwenye daladala.
Kwenye hili mmetuponza, siku hizi ukimpokea anashuka bila taarifa na kukuachia mtoto moja kwa moja, katika dunia yetu msaada umegeuka msala.
Naendelea kuzingatia na kukumbuka usio wa wahenga, waliotaka nisaidie wenye uhitaji hasa ninapowaona wanaomba barabarani. Niwaambie tu, katika karne ya 21 wanaoomba wengi wanatumikishwa na wenye uwezo wao tena kwa ujira kiduchu, gazeti la Mwananchi liliwahi kuandika.
Hayo tu yamewashangaza? kuna hili…, pamoja na kile nilichoambiwa kwamba watu wakifikisha umri fulani hufunga ndoa inayohusisha mume na mke. Siku hizi haiko hivyo, eti John anamuoa Daniel na hata Salum anamuoa Hassan.
Nautamani wakati ule babu, mvua ikinyesha tunafurahia kuandaa mashamba kwa ajili ya kupanda mazao, hivi nikwambie? Siku hizi ikinyesha tunasherehekea kwa kutafuta wenza wa mkataba, tena wanapatikana kwa Sh3,000 hadi Sh5,000.
Usishangae babu, thamani ya fedha hiyo inakuwezesha kuchagua unayemuhitaji, aghalabu hujipanga pembezoni mwa barabara na karibu na kumbi za starehe, unajichagulia.
Babu, ulipenda kunambia asiyefunzwa na mamae atafunzwa na ulimwengu. Siku hizi wamefunzwa na mama, ulimwengu na wamehitimu, nadhani wamekosa vyeti.
Ngoja nikuthibitishie, kuviona viungo vinavyopaswa kufichwa kwenye mwili hasa wa mwanamke, ni rahisi siku hizi kama ilivyo kuwaona watu Kariakoo. Wanavalia mavazi mithili ya chandarua kukurahisishia kuona.
Mtindo wa maisha ya sasa babu, unaibua haja ya kuyaacha uliyonifunza angalau niishi kwa namna mpya kuendana na karne hii.
Mtazamo wa kisaikolojia kuhusu aina na mtindo wa maisha ya sasa ni kuendana na hali halisi kama inavyofafanuliwa na Mtaalamu wa Kada hiyo, Magolanga Shagembe.
Shagembe ambaye pia ni Mhadhiri wa Saikolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), anasema ili kuishi vema katika karne ya 21, hauna budi kuendana na uhalisia.
Lakini kuendana huko, anasema kusitoe mwanya wa kujihusisha na utamaduni mpya unaoathiri ustawi au heshima yako.
“Ikitokea unamsalimia mtu mzima kwa kumwambia shikamoo anaitika vinginevyo, kwa sasa jaribu kumsalimia kwa salamu anayoihitaji.
“Lakini ukiona aina ya salamu anayohitaji inahusisha mambo mengine yasiyostahili, mbadilishie salamu au tengeneza mazingira ya kumuepuka,” anasema.
Ili kuepuka migongano na jamii, anashauri vema kuepuka kuzingatia mabadiliko unayokutana nayo, badala yake utafute namna ya kuishi kuendana nayo bila kuathirika. |
Licha ya Dar es Salaam kuonekana Jiji pendwa na watu, hivi unajua kuwa Pwani ndiyo Mkoa kimbilio la | Licha ya Dar es Salaam kuonekana Jiji pendwa na watu, hivi unajua kuwa Pwani ndiyo Mkoa kimbilio la wengi nchini?
Kwa taarifa yako, katika mwaka 2022 jumla ya watu 667,676 walikimbilia Pwani, huku 142,910 wakifungasha virago kulihama Jiji la Dar es Salaam.
Kulingana na taarifa ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, idadi ya watu imeongezeka katika Mkoa wa Pwani kutoka milioni 1.35 mwaka 2021 hadi milioni 2.02 mwaka jana.
Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 32.
Wakati Pwani hali ikiwa hivyo, Dar es Salaam kwenyewe mambo si mazuri, kwani idadi ya watu imepungua kutoka milioni 5.5 mwaka 2021 hadi watu milioni 5.3 mwaka 2022.
Hiyo ni sawa na kupungua kwa asilimia 2.6
Kwa muktadha wa kiuchumi, kulingana na wanazuoni wa kada hiyo, ongezeko la watu Pwani lina faida na hasara, kadhalika vivyo hivyo kwa upande wa Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa wataalamu wa uchumi, gharama kubwa za kupanga vyumba na nyumba ni miongoni mwa sababu zinazowahamisha watu Dar es Salaam, huku kuboreshwa kwa miundombinu na wingi wa fursa ndiyo kunakoifanya Pwani kuwa kimbilio.
Wasemavyo wachumi
Kuongezeka kwa gharama za maisha katika Jiji la Dar es Salaam ni moja ya sababu inayotajwa kuwahamisha watu kutoka eneo hilo kwenda kwingineko, kama inavyoelezwa na Mhadhiri Msaidizi wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Maria Erasmus.
Kulingana na Maria, gharama za malazi katika Jiji la Dar es Salaam ndizo hasa zilizoongezeka maradufu, hali inayowafanya baadhi ya watu kushindwa kumudu maisha.
“Bei ya kupanga nyumba au chumba Dar es Salaam ni kubwa mno kwa maisha ya kawaida ni changamoto, watu wanashindwa kuishi kwa sababu hiyo,” alieleza.
Kuhusu Pwani, alisema maendeleo ya miundombinu ndiyo sababu ya watu kukimbilia mkoani humo.
“Sasa hivi mwendokasi inafika hadi Pwani mtu anaweza kuishi Pwani na akafanya kazi Dar es Salaam na kila siku akafanya safari bila tatizo,” alisema.
Ongezeko la fursa za kiuchumi katika Mkoa wa Pwani, ni sababu nyingine inayotajwa na Maria kuchagiza watu kuhamia.
“Kuna viwanda vingi kule Pwani kwa hiyo hizo zote ni fursa watu wanahamia eneo kufuata fursa, ukiona wameongezeka ujue na fursa zimeongezeka,” alisema.
Hata hivyo, alisema ongezeko la watu katika eneo fulani ni tija kwa kuwa linaongeza shughuli za uzalishaji kutokana na wingi wa nguvu kazi.
“Faida nyingine ni kukua kwa shughuli za biashara kwa sababu wanunuzi wanaongezeka kwa hiyo Pwani inafaidika kwa hilo,” alieleza.
Mtafiti wa masuala ya uchumi, Thobias Shija alisema ongezeko hilo la watu katika Mkoa wa Pwani, pamoja na faida lakini zipo hasara zake.
Panapo watu wengi, alieleza gharama za maisha huongezeka kwa kuwa wafanyabiashara hutumia idadi hiyo kama ongezeko la soko, hivyo bei zitapanda.
Akifafanua hilo, Shija alisema ongezeko la gharama za nyumba na vyumba katika Jiji la Dar es Salaam, limechagizwa na idadi kubwa ya watu walioongeza mahitaji.
“Kwa hiyo hali kama hiyo inaweza kuukumba Mkoa wa Pwani, kwa kadri watu wanavyoongezeka mahitaji yanaongezeka na wafanyabiashara wanapandisha bei.
“Mfano Dodoma kabla ya Serikali kuhamia huko bei ya vyumba na nyumba ilikuwa ndogo lakini sasa ambapo Serikali imehamia huko, nyumba na vyumba vya kupanga vimeongezeka bei,” alisema.
Kuhusu kupungua kwa watu jijini Dar es Salaam, Shija alisema kutapunguza gharama za maisha kwa upande mmoja, lakini kutasababisha hasara kwa wafanyabiashara kwa upande mwingine.
“Watu wanapopungua masoko yanapungua, wale waliokuwa wanafanya biashara kama za kupangisha nyumba wapangaji watapungua, maana yake watalazimika kushusha bei ili wapate wateja, hiyo itawatia hasara,” alisema.
Lakini jambo hilo hilo, alilitaja ni faida kwa wakazi wa Dar es Salaam akifafanua kwa kadri wafanyabiashara watakavyoshusha bei kutokana na kupungua kwa soko na ndivyo wananchi watakavyomudu gharama.
“Mfanyabiashara anaumia, mwananchi anafurahia kwa hiyo hii inamuumiza mmoja na mwingine anafurahia,” alieleza.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila alisema kwa ugeni wake ni vigumu kufafanua lolote.
"Kwa ugeni wangu naendelea kujifunza haraka mambo mengi ikiwemo hayo maswali yako," alijibu Chalamila. |
‘Muungwana akivuliwa nguo huchutama’ ndiyo usemi unaoakisi kilichofanywa na mfanyabiashara, Rostam A | ‘Muungwana akivuliwa nguo huchutama’ ndiyo usemi unaoakisi kilichofanywa na mfanyabiashara, Rostam Aziz baada ya kukiangukia Chama cha Majaji Tanzania (JMAT), akikiomba radhi kutokana na kauli yake iliyotafsiriwa kuidharau mahakama.
Rostam aliitoa kauli hiyo, Juni 26, mwaka huu wakati anafafanua kuhusu Mkataba wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai (IGA), kuhusu uwekezaji na uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, mbele ya waandishi wa habari.
Katika maelezo yake kuhusu kifungu cha IGA kinachotaka migogoro baina ya pande hizo kutatuliwa kwa sheria za Uingereza nchini Afrika Kusini, Rostam alisema, "hakuna mwekezaji atawekeza kwenye nchi ambayo kesi ikipelekwa hapo Kisutu kiongozi yoyote anaweza kupiga simu akaielekeza mahakama nini cha kufanya.”
Kutokana na kauli hiyo, JMAT jana ilitoa taarifa kwa umma, ikimtaka ama athibitishe madai ya Maofisa wa mahakama wanaopokea maelekezo kutoka kwa viongozi wa Serikali kufanya uamuzi au aombe radhi hadharani.
Inaonekana, Mfanyabiashara huyo amechagua kuchutama, baada ya jana jijini Dar es Salaam, kuzungumza mbele ya wanahabari kuwa haikuwa dhamira yake kutoa kauli hiyo.
Hata hivyo, Rais wa JMAT, Jaji John Kahyoza alikiri kupokea msamaha wa Rostam na kwamba chama hicho hakina tena tatizo naye.
“Tumepokea msamaha wake, mtu akiomba msamaha kwa kawaida husamehewa, kwa hiyo tumemsamehe na hatuna tatizo naye tena,” alisema.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Rostam alisema halikuwa kusudio lake kuidharau mahakama bali kauli hiyo ni kama kutereza kwa ulimi.
"Kwa sababu ya kutambua na kuheshimu dhima, hadhi na wajibu wa kikatiba wa mahakama, ningependa kusema yafuatayo.
"Nilitereza ulimi, maana kusudio langu lilikuwa ni kueleza kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba ili tupate uwekezaji nchini hatuna budi kuendana na taratibu zinazoendana," alisema.
Dhamira yake katika kauli hiyo, Rostam alisema ni kuuelimisha umma kuhusu wale wanaosema ni kinyume cha taratibu, sheria za Uingereza kutumika katika usuluhishi wa mgogoro wa IGA.
Hata hivyo, alifafanua kwa kuwa Tanzania ni mwanachama wa Exit inayoongoza uwekezaji katika mataifa yote duniani, utaratibu wa kutumika sheria za kimataifa katika usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji kati ya nchi na nchi ni sharti utekelezwe.
"Kama nimekwaza sehemu yoyote ile, naomba nieleweke hivyo kwamba ulikuwa uterezaji wa ulimi nilivyokuwa najaribu kufafanua kuhusu uwekezaji," alisema.
Alisema ni vigumu kupata wawekezaji iwapo nchi haitafuata sheria za kimataifa katika utatuzi wa migogoro.
"Na sheria ya Exit ipo wazi kabisa kwamba mwekezaji anapopata tatizo mnakwenda eneo ambalo majaji hawafungamani na upande wowote," alisema. |
Haikuchukua muda mrefu kwa bilionea, Rostam Aziz kukiomba radhi Chama cha Majaji Tanzania (JMAT), ku | Haikuchukua muda mrefu kwa bilionea, Rostam Aziz kukiomba radhi Chama cha Majaji Tanzania (JMAT), kutokana na kauli yake iliyotafsiriwa kuidharau mahakama.
Rostam alitoa kauli hiyo, Juni 26, mwaka huu katika mkutano wake na waandishi wa habari kuhusu Mkataba wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai (IGA), kuhusu uwekezaji na uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam.
Katika maelezo yake kuhusu kifungu cha mkataba huo kinachotaka migogoro baina ya pande hizo kutatuliwa kwa sheria za Uingereza nchini Afrika Kusini, Rostam alisema, "hakuna mwekezaji atawekeza kwenye nchi ambayo kesi ikipelekwa hapo Kisutu kiongozi yoyote anaweza kupiga simu akaielekeza mahakama nini cha kufanya.”
Kutokana na kauli hiyo, JMAT jana kilitoa taarifa kwa umma, kikimtaka ama athibitishe madai ya Maofisa wa mahakama wanaopokea maelekezo au aombe radhi hadharani.
Inaonekana, Mfanyabiashara huyo amechagua kuomba radhi, baada ya jana jijini Dar es Salaam, kuzungumza mbele ya wanahabari kuwa haikuwa dhamira yake kutoa kauli hiyo.
Kulingana na Rostam, halikuwa kusudio lake kuidharau mahakama bali kauli hiyo ni kama kutereza kwa ulimi.
"Kwa sababu ya kutambua na kuheshimu dhima, hadhi na wajibu wa kikatiba wa mahakama, ningependa kusema yafuatayo.
"Nilitereza ulimi, maana kusudio langu lilikuwa ni kueleza kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba ili tupate uwekezaji nchini hatuna budi kuendana na taratibu zinazoendana," alisema.
Dhamira yake katika kauli hiyo, Rostam alisema ni kuuelimisha umma kuhusu wale wanaosema ni kinyume cha taratibu, sheria za Uingereza kutumika katika usuluhishi wa mgogoro wa IGA.
Hata hivyo, alifafanua kwa kuwa Tanzania ni mwanachama wa Exit inayoongoza uwekezaji katika mataifa yote duniani, utaratibu wa kutumika sheria za kimataifa katika usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji kati ya nchi na nchi ni sharti utekelezwe.
"Kama nimekwaza sehemu yoyote ile, naomba nieleweke hivyo kwamba ulikuwa uterezaji wa ulimi nilivyokuwa najaribu kufafanua kuhusu uwekezaji," alisema.
Alisema ni vigumu kupata wawekezaji iwapo nchi haitafuata sheria za kimataifa katika utatuzi wa migogoro.
"Na sheria ya Exit ipo wazi kabisa kwamba mwekezaji anapopata tatizo mnakwenda eneo ambalo majaji hawafungamani na upande wowote," alisema. |
Siku tisa baada ya mfanyabiashara, Rostam Azizi kushuku uhuru wa Mahakama ya Kisutu, Chama cha Majaj | Siku tisa baada ya mfanyabiashara, Rostam Azizi kushuku uhuru wa Mahakama ya Kisutu, Chama cha Majaji Tanzania (JMAT) kimemjia juu kikimtaka athibitishe tuhuma alizozitoa dhidi ya mahakama hiyo.
Rostam aliishuku mahakama hiyo Juni 26, mwaka huu alipozungumzia sakata la bandari akisema, “hakuna mwekezaji atawekeza kwenye nchi ambayo kesi ikipelekwa hapo Kisutu kiongozi yoyote anaweza kupiga simu akaielekeza mahakama nini cha kufanya.”
Kutokana na kauli yake hiyo, iliyotafsiriwa kuwa ni kuidharau mahakama JMAT imechapisha taarifa kwa umma leo, Julai 4, 2023 kikimtaka mfanyabiashara huyo athibitishe kauli yake.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, chama hicho hakikuwahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha maofisa wa mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa uamuzi katika mahakama hiyo.
“Kutokana na maelezo hayo, tumesikitishwa na kauli ya Rostam Aziz ambaye hatukutarajia aongee mambo mazito kama hayo bila kuwa na uhakika wala uthibitisho,” imeeleza taarifa hiyo.
JMAT kupitia taarifa hiyo, imesema kauli za mfanyabiashara huyo zinahatarisha uhusiano na ushirikiano kati ya mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi.
“Tunaomba wananchi wenye nia njema na mahakama na mihimili mingine waendelee kuwa na imani na mfumo wa utoaji haki nchini," im”eleza.
Aidha, chama hicho kimemtaka mfanyabiashara huyo kuthibitisha kauli hiyo na akishindwa, anapaswa kutumia jukwaa alilotolea taarifa hiyo kuomba radhi.
“Anapaswa athibitishe kauli yake akibainisha jina la Jaji na lini alipewa maagizo na Serikali kutoa maamuzi kinyume na taratibu zilizopo.
“Akishindwa kutoa uthibitisho, tunamtaka atumie jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule,” amesema. |
Wananchi milioni 51.3 katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wanakabiliwa na c | Wananchi milioni 51.3 katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wanakabiliwa na changamoto ya usalama duni wa chakula.
Hiyo ni kulingana na tathmini iliyofanywa mwaka 2020/21 na kwamba idadi hiyo ni sawa na asilimia 13.5 ya wakazi wote milioni 380 wa SADC.
Kadhalika, idadi hiyo ni ongezeko la asilimia 25.7 kutoka tathmini iliyofanyika katika mwaka 2019/20, ikionyesha kasi ya changamoto ya usalama wa chakula katika nchi za ukanda huo.
Hili linatokea wakati, ukanda huo ukiwa na takriban mita za mraba milioni 9.85 zinazofaa kwa shughuli za kilimo na zina uwezo wa kuzalisha chakula kuilisha Afrika na kwingineko.
Hayo yalielezwa jijini Arusha jana na Rais Samia Suluhu Hassan, alipohutubia mkutano wa 53 wa wabunge wa SADC, uliolenga kujadili kuhusu usalama wa chakula, kilimo na usawa wa jinsia.
Katika hotuba yake hiyo, Rais Samia alisema, “Hii haikubaliki, hali hii inasababishwa na machafuko ya dunia na mabadiliko ya tabianchi hasa yanayoathiri sekta ya kilimo.”
Mkuu huyo wa nchi, aliyekuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo, alieleza ni wakati kwa nchi wanachama wa SADC kuanza kutekeleza sera na mikakati zilizojiwekea.
“Tunakuja na sera na mikakati mbalimbali lakini hatutekelezi, sasa huu ni wakati wa kuzungumza na kuanza kutekeleza,” alisema.
Kwa mujibu wa Rais Samia, alisema ukanda huo unapaswa kufanya kadri uwezavyo kuhakikisha unazalisha chakula salama na kuilisha Afrika na kwingineko.
“Tuna ardhi muhimu kwa ajili ya kilimo lakini tunapaswa kuhakikisha ardhi hii inazalisha chakula kuziba pengo linalofanya nchi za SADC kuwa na njaa,” alisema.
Namna njema ya kufanikisha hilo, alisema ni utekelezaji wa sera mbalimbali na mikakati inayowekwa mara kwa mara kama ule wa mwaka 2015 wa SADC.
Ili kukabiliana na changamoto mbalimbali, alisema mabunge ya nchi wanachama yana kazi kubwa ya kufanya kubadilisha sera mbalimbali za kilimo.
Kuhusu usawa wa jinsia, aliwataka viongozi wote kuendelea na jitihada na kupaza sauti zao kuhakikisha haki inatendeka.
“Tumejitambulisha katika ulingo mwaka 1995 na mengi yamebadilika, bila hayo Samia Suluhu asingesimama hapa leo kama Rais wa Tanzania,” alisema.
Mwenyekiti wa Kokasi ya Wanawake katika nchi za SADC, Regina Esparon alisema nguvu ya ziada inahitajika kufanya mapinduzi katika usawa wa jinsia kwenye uongozi.
Kauli yake hiyo inatokana na kile alichoeleza kuwa, takwimu za African Barometer zinaonyesha ni asilimia 22 pekee ya wanawake ndiyo wanaoshika nafasi za uongozi katika nchi za Afrika.
“Kunahitajika nguvu ya ziada na mbinu za kimapinduzi ili kuwawezesha wanawake na hatimaye waongezeke katika uongozi wa kisiasa,” alisema.
Katika hotuba yake hiyo, aliipongeza Tanzania kwa kuwa mfano wa kuwa na Rais mwanamke, akisema uongozi wake umekuwa kielelezo cha uwezo wa wanawake katika kuongoza.
“Uongozi wake ni kielelezo cha mafanikio ambayo mwanamke akiaminiwa na kupewa nafasi atayafikia mbali na changamoto za jinsia yake,” alisema.
Alisisitiza uwezeshwaji wa wanawake hata katika shughuli za kilimo, akifafanua ndilo kundi linalofanya kazi kubwa, lakini linakabiliwa na changamoto ya uwezeshaji.
Alitaja vikwazo vinavyowakabili wanawake ni umiliki ardhi, elimu ya kilimo na rasilimali nyingine wezeshi kwa uzalishaji.
Kama wanawake, alieleza wana wajibu wa kuhakikisha vikwazo hivyo vinatatuliwa ili kuwapa nafasi wanawake wawe na mchango katika sekta ya kilimo katika nchi za SADC.
“Kuwawezesha wanawake katika kilimo ni jambo jema litakalokuza usalama wa chakula katika nchi zetu za SADC,” alisema.
Pamoja na kuwahusisha wanawake katika kilimo, alisema ni vema pia wahusishwe kwenye kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. |
Rais Samia Suluhu Hassan amesema licha ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ( | Rais Samia Suluhu Hassan amesema licha ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujiwekea mikakati na sera za kuboresha sekta ya kilimo, bado zinatajwa kuwa na njaa.
Amesema ni wakati sasa nchi hizo zitumie mikakati na sera hizo ili kuufanya ukanda wa SADC kuwa mzalishaji na msambazaji mkubwa wa chakula Afrika na kwingineko.
Rais Samia ametoa kauli hiyo leo, Julai 3, 2023 katika mkutano wa 53 wa Jumuiya ya Wabunge wa nchi za SADC uliofanyika jijini Arusha.
Kulingana na mkuu huyo wa nchi aliyealikwa kuwa mgeni rasmi, nchi za SADC zina kilometa za mraba milioni 9.85 zinazoweza zinazofaa kwa shughuli ya kilimo.
“Kama zitatumiwa vema. Tuna ardhi muhimu kwa ajili ya kilimo lakini tunapaswa kuhakikisha ardhi hii inazalisha chakula kuziba pengo linalofanya nchi za SADC kuwa na njaa,” amesema.
Namna njema ya kufanikisha hilo, amesema ni utekelezaji wa sera mbalimbali na mikakati inayowekwa mara kwa mara kama ule wa mwaka 2015 wa SADC.
“Tunakuja na sera na mikakati mbalimbali lakini hatutekelezi, sasa huu ni wakati wa kuzungumza na kuanza kutekeleza,” amesema.
Ili kukabiliana na changamoto mbalimbali, amesema mabunge ya nchi wanachama yana kazi kubwa ya kufanya kubadilisha sera mbalimbali za kilimo.
Kuhusu usawa wa jinsia, amewataka viongozi wote kuendelea na jitihada na kupaza sauti zao kuhakikisha haki inatendeka.
“Tumejitambulisha katika ulingo mwaka 1995 na mengi yamebadilika, bila hayo Samia Suluhu asingesimama hapa leo kama Rais wa Tanzania,” amesema. |
Tamati ya maisha ya mwanaume mmoja imefikia jana wilayani Moshi, baada ya kuuawa wakati akifanya map | Tamati ya maisha ya mwanaume mmoja imefikia jana wilayani Moshi, baada ya kuuawa wakati akifanya mapenzi katika moja ya uchochoro mkoani Kilimanjaro.
Mwanaume huyo ambaye hadi sasa jina lake halijafahamika, aliuawa kati ya saa 8 na 9 usiku, alipokuwa anafanya kitendo hicho na mmoja wa wanawake wanaofanya biashara ya ngono.
Taarifa za kifo chake, zimethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Simon Maigwa aliyesema tayari mtuhumiwa mmoja anashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano.
“Mtuhumiwa mkuu tumeshamkamata tunamfanyia mahojiano, lakini taarifa zaidi nitatoa kesho (leo) zikiwa zimekamilika.
“Wameuwana wakiwa wanagombea changudoa huku, unajua hawa vijana wetu bwana, kesho (leo) nitatoa taarifa zaidi,” alisema Maigwa.
Hata hivyo, kamanda huyo hakufafanua kile kinachodaiwa na baadhi ya mashuhuda kwamba, aliyeuawa ni mwanafunzi au muuguzi, kwa kile alichosisitiza kuwa taarifa zaidi atatoa leo.
Eneo alikouawa mwanaume huyo lililopo Mtaa wa Rengua Manispaa ya Moshi, linatajwa kuwa maarufu kwa kufanyika ngono hadharani.
Gazeti hili mwaka 2020, liliwahi kuandika kuhusu shughuli zinazofanyika katika uchochoro huo, unaokadiriwa kuwa na urefu wa mita 60.
Eneo hilo linalopakana na Maktaba ya Mkoa kutokea barabara ya Rengua, limezungukwa na kumbi za starehe na mitaa kuelekea kumbi hizo ndiyo inayotumika na wafanyabiashara ya ngono kufanya shughuli hiyo.
“Mimi nilikuwa hapa ni kuwa usiku wa kuamkia leo (Jana), huyo jamaa alienda kuchukua dada poa pale nje kwenye hiyo klabu. Huyo demu (mwanamke) akampeleka jamaa kwenye huo uchochoro,” alieleza mmoja wa madereva bodaboda katika eneo hilo.
Inavyoonekana, alisema changudoa huyo alikuwa na mwanaume anayefanya shughuli za bodaboda na alipomuona mwanamke wake na mtu mwingine alipata wivu uliomsababisha kufanya tukio hilo.
“Sasa inavyoonekana huyo demu ana jamaa yake ni dereva bodaboda mwenzetu kwa hiyo inavyoonekana alipata wivu japo anajua demu wake ni changudoa ndio wakaenda wakamchoma visu wakati akiendelea kufanya mapenzi,” alieleza.
Utata kuhusu shughuli ya aliyeuawa unatokana na kile akilichoelezwa na mashuhuda kuwa, baada ya tukio vilionekana vitambulisho viwili kikiwemo cha mwanafundi wa chuo na mtumishi wa umma.
“Kwa kweli polisi ndio wanaweza kusema ni mwanafunzi au mkunga muuguzi maana alikuwa na vitambulisho viwili ambavyo niliviona,” kilidokeza kimoja na chanzo kilichoshuhudia tukio hilo. |
Umewahi kujiuliza lolote kuhusu mkataba wa ushirikiano (IGA) wa uwekezaji na uboreshaji bandari ya D | Umewahi kujiuliza lolote kuhusu mkataba wa ushirikiano (IGA) wa uwekezaji na uboreshaji bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai?
Unapata maswali yasiyojibika kuhusu mkataba huo au hofu juu ya kile kinachoelezwa na wengi kwamba mkataba huo ni sawa na kuiuza bandari ya Dar es Salaam?
Gazeti hili linakuja na jawabu la kila unachojiuliza kuhusu mkataba huo, baada ya kufanya mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa.
IGA ni nini?
Miongoni mwa hoja kubwa ni mkataba wenyewe na uhusiano wake na mikataba ya utekelezaji.
Katika hili Mbossa anasema IGA ni makubaliano ya ushirikiano kati ya Serikali mbili au Zaidi, aghalabu hulenga kujenga ushirikiano katika uchumi, biashara na jamii kwa pande husika.
Makubaliano hayo, kwa mujibu wa Mbossa, huwezesha taasisi za kisekta za nchi husika kuingia mikataba ya utekelezaji kwa manufaa ya pande zote.
“Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, IGA inatakiwa kuwasilishwa na kuridhiwa na Bunge. Kuridhiwa kwa mkataba huu kunaipa Serikali idhini ya kufanya majadiliano na kusaini mkataba wa uwekezaji (HGA) na mwekezaji mtarajiwa,” anasema.
Kwa mujibu wa Mbossa, HGA ndio mkataba unaoainisha matakwa na matarajio ya jumla ya pande zote, kadhalika unatoa mwongozo wa masuala mbalimbali yakiwemo maeneo ya uwekezaji, ushirikiano na ajira.
Maeneo mengine aliyoyataja ni mafunzo kwa wafanyakazi, uhamishaji wa teknolojia, masuala ya ardhi, utunzaji wa mazingira, faida ya uwekezaji kwa jamii na kodi.
Anasema kusainiwa kwa HGA kunaruhusu mwekezaji kuingia mkataba au mikataba mahsusi ya utekelezaji wa uwekezaji na taasisi au mamlaka husika za Serikali.
Katika kuhakikisha Tanzania inapata tija stahiki kupitia huduma za bandari, anasema Oktoba 25, mwaka jana, Serikali ya Tanzania na Dubai zilisaini IGA ikilenga uendelezaji na uboreshaji wa utendaji kazi wa bandari.
“Kwa ufafanuzi huo, ieleweke kuwa mpaka sasa hakuna mkataba wa uwekezaji HGA kati ya Serikali ya Tanzania na Mwekezaji DP World na wala hakuna mkataba wa utekelezaji wa uwekezaji kati ya TPA na DP World,” anasema.
Je, Bandari imeuzwa?
Kutokana na kusainiwa kwa IGA, kumeibuka mitazamo kuwa bandari inauzwa, katika hilo Mbossa anafafanua hakuna kitakachouzwa.
Kinachofanyika anasema ni ukodishaji wa uendeshaji wa bandari kwa kampuni binasfi, huku Serikali kupitia TPA itabaki kuwa mmiliki na kuachana na shughuli za uendeshaji.
“Shughuli za uendeshaji ndizo zinazokodishwa kwa DPW. Mfano mzuri wa kinachofanyika ni kama mtu anavyojenga hotel kisha akaikodisha kwa mwendeshaji mwingine kwa makubaliano maalum,” anasema.
Hofu ya usalama
Kwa kuwa bandari ni mpaka, mtazamo wa wengi ni kwamba kuendeshwa na kampuni ya kigeni kunaweka rehani usalama wan chi.
Akijibu hilo, Mkurugenzi huyo anasema usalama wa bandarini unasimamiwa kwa mujibu wa sheria za ndani ya nchi na zile za kimataifa zinazohusu masuala ya ulinzi na usalama.
“Sheria za ndani ya nchi zinasimamia ulinzi katika nyanja mbili ambazo ni ulinzi wa ndani ya bandari na ulinzi wa nje ya bandari. Ulinzi wa ndani husimamiwa na askari wa bandari na huwa katika malango yote ya kuingia na kutoka bandarini,” anasema.
Ulinzi wa jumla, anasema husimamiwa na vyombo mbalimbali vya usalama vilivyopo bandarini kwa mujibu wa sharia, likiwemo Jeshi la Wananchi (JWTZ), Usalama wa Taifa, Uhamiaji, Polisi na vyombo vingine vya usalama.
Kuhusu sheria za kimataifa, anasema Bandari ya Dar es Salaam inatumia ISPS Code ambayo, pamoja na mambo mengine ya kiusalama, inazitaka meli zote zinazoingia bandarini kutoa taarifa zake kwa TPA.
“Taarifa hizi hutumiwa na TPA kuweka usalama “security levels” zitakazotumika kwa ajili ya meli husika. Security Level hutegemea “eminent security threat” ya nchi meli hiyo inapotoka au ilikopitia,” anasema.
Hata hivyo, anasema mikataba ya uwekezaji haiondoi mamlaka ya Serikali katika masuala ya ulinzi, akitolea mfano kampuni ya Swissport iliyopo viwanja vya ndege lakini usalama na ulinzi umebaki kwa Serikali.
Je! Mwekezaji amepewa bandari zote nchini?
Kwa sababu kilichosainiwa ni IGA, Mbossa anasema hakuna bandari yoyote hadi sasa ambayo mwekezaji huyo amepewa.
Anasema mkataba wa ushirikiano ambayo pande husika zimeingia, kisheria haumpi mwekezaji eneo lolote, bali unafugua milango ya majadiliano juu ya mikataba ya uwekezaji (HGA) na ile ya utekelezaji.
“Kwa lugha nyepesi IGA ni sawa na kishika uchumba. Unapopeleka barua ya posa sio lazima utamuoa unayemposa. Ndoa itategeana na makubaliano mengine baina ya wanaotarajia kuoana ikiwa ni pamoja na makubaliano ya mahali,” anasema.
Hata hivyo, anasema Ibara ya 2 ya IGA inaweka msingi wa makubaliano ambao ni uedelezaji, uboreshaji, usimamizi na uendeshaji wa bandari za mwambao wa bahari na maziwa.
“Ibara hii haitoi wajibu kwa upande wowote kuteleza suala lolote katika hayo. Ili kujua wajibu wa pande za mkataba, maelezo yapo katika Ibara ya 5 (1), ambayo inaeleza kwamba DPW atakuwa na haki ya pekee ya kuendeleza, kusimamia na kuendesha maeneo yote yaliyoorodheshwa katika Kiambatisho Na. 1,” anasema.
Anakifafanua kiambatanisho hicho ni DPW ataendeleza, kusimamia na kuendesha “RoRo Terminal (Berth 0), Genaral Cargo Terminal (Berth 1-4) na Container Terminal (Berth 5-7) za Bandari ya Dar es Salaam. Kwa hiyo majadiliano ya HGA na Mikataba ya utekelezaji yatajikita katika maeneo hayo.
“Kwa hiyo hakuna sehemu yoyote kwenye Mkataba wa IGA inayosema DPW atachukua Bandari zote za Tanzania,” anasema.
Migogoro itatatuliwa wapi, kwa sharia gani?
Anasema kwa mujibu wa Sheria ya Maliasili ya mwaka 2017 kifungu cha 11(1) na (2) vinaweka wazi kuhusu hilo.
Kwa mujibu wa maelekezo ya sheria hiyo, anasema migogoro inayolazimika kutatuliwa na mahakama au vyombo vingine vya sheria vya Tanzania ni ile inayotokana na uchimbaji, uvunaji au utwaaji na utumiaji wa Rasilimali asilia.
“Sasa, kama nilivyokwishafafanua hapo juu, IGA ni mkataba unaoanzisha ushirikiano kati ya nchi na nchi katika nyanja na masuala wanayokubaliana kushirikiana.
“IGA sio mkataba wa uchimbaji, uvunaji au utwaaji na utumiaji wa rasilimali bali IGA inaporidhiwa na Bunge ndio inayotoa ridhaa ya Serikali kuingia mikataba ya uchimbaji, uvunaji au utwaaji na utumiaji wa rasilimali. IGA yenyewe sio miongoni mwa mikataba hiyo,” anasema.
Ndio maana, anasema katika mkataba huo Ibara ya 21 inasema migogoro yote itakayotokana na vipengele vya IGA itatatuliwa kwa mujibu wa Sheria za Uingereza.
“Wakati huohuo migogoro itayotokana na mikataba ya HGA na ile ya utekelezaji yaani utwaaji na utumiaji wa Bandari itatatuliwa kwa Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” anasema.
Anasema kwa kuwa IGA inalinda mahusiano ya taifa na taifa migogoro inayotokana na vipengele vyake haiwezi kutatuliwa na Mahakama za taifa mojawapo kati ya mataifa yenye mgogoro.
“Kwa hiyo mgogoro wa aina hii daima hutatuliwa na vyombo vya kisheria vya taifa jingine lisilofungamana na upande wowote wa mkataba husika (IGA).
Hii ndio sababu ya migogoro itakayotokana na IGA kwenda kutatuliwa nchini Afrika ya Kusini. Ifahamike kuwa Afrika ya kusini ni kwa ajili ya migogoro inayotokana na IGA peke yake na haihusiani na migogoro inayotokana na mikataba ya utekelezaji. Rejaea Ibara ya 20(2)(e) na 20(3) za IGA,” anasema.
Je, Mkataba hauwezi kufanyiwa marekebisho?
Anasema suala hilo limeelezewa katika Ibara ya 22 ya IGA iliyoweka bayana kuwa mkataba unaweza kufanyiwa marekebisho wakati wowote pande mbili zitakapokubaliana.
Je, kweli mkataba huu hauna ukomo?
Mbossa anasema ukomo wa mkataba huo umeelezwa katika Ibara ya 23(1) ya IGA ambayo inasema mkataba utafikia ukomo pale ambapo suala lolote kati ya masuala kadhaa yatatokea.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, masuala hayo ni kuisha kwa shughuli za mradi, kufikia ukomo kwa HGA na mikataba mingine ya utekelezaji.
Kwanini haukushindanishwa, kutangazwa?
Anasema suala hilo, lina sababu mbalimbali ukiwemo uzoefu na umahiri wa DPW katika uendeshaji wa Bandari.
“DPW anaendesha jumla ya bandari 190 duniani zilizopo katika nchi 68. Pia anahudumia takribani asilimia tisa ya shehena yote ya makasha inayosafirishwa duniani.
“Kwa upande wa Afrika DPW ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika nchi zipatazo sita amazo ni Algeria, Somalia, Senegal, Angola, Msumbiji na Rwandam” anasema.
Lakini sababu ya pili, anasema sheria ya manunuzi ya mwaka 2011 ndiyo inayotoa masharti ya kutangaza na kushindanisha zabuni ili kupata washitiri.
“Pamoja na utaribu wa kushindanisha, sheria hiyo inatoa njia nyingine zinazoweza kutumika katika manunuzi kama vile restricted method, single source procurement na direct procurement,” anasema.
Anasema njia hizo zipo kisheria na zinaruhusiwa kutumika kulingana na sababu zinazomfanya mnunuzi kuchagua njia moja na kuiacha nyingine.
“Kwa mfano, ukinunua vifaa vya kijeshi huwezi kutangaza. Kutokana na sababu zilizoelezwa na sababu za kiinteligensia ya masoko na vita za kiuchumi, Serikali ililazimika kutumia njia ya Single Source ili kumpa zabuni DPW,” anasema.
Je! Wafanyakazi wa TPA watapoteza ajira zao?
Anasema masuala ya ushirikishwaji wa wazawa na ajira yamezingatiwa katika Ibara ya 13 ya mkataba wa IGA.
Kulingana na ibara hiyo, anasema DPW anatakiwa kuhifadhi ajira za wafanyakazi wa TPA, kununua bidhaa na huduma za Tanzania, kusaidia katika masuala ya mafunzo na utafiti kuhusiana na shughuli za kibandari.
Kujitoa, kuvunja au kusitisha mkataba
Katika maelezo yake Mbossa anasema ibara ya 23 ina ibara ndogo nne zinazotakiwa kusomwa kwa pamoja.
“Ukisoma ibara ndogo ya kwanza (1), ya pili (2) na ya tatu (3) utaona kuwa mkataba unaweza kuvunjwa baada ya pande zote kuwa zimeridhia.
“Pia ibara ndogo ya kwanza inatoa ukomo wa mkataba na mazingira yatayofanya mkataba huo wa IGA ufikie ukomo. Ibara ndogo ya (2) inasema kama HGA itavunjwa kabla ya kufikia ukomo, Mkataba wa (IGA) itaendelea kwa muda kwa lengo la kuruhusu upande utakaokuwa umeathirika kudai haki zake kama zitakuwepo na upande mwingine kutimiza wajibu wake utakaokuwepo,” anasema.
Katika mazingira hayo, anasema ibara ndogo ya nne inalinda haki za wahusika katika mikataba ya utekelezaji.
“Kwa kuwa IGA ndio mkataba mama, ukivunjika wenyewe na ile migogoro yote inakuwa imekwisha. Yumkini, Serikali zikakosana kidiplomasia lakini TPA na DPW hawajakosana, ukiruhusu IGA ivunjwe moja kwa moja TPA na DPW watalazimika kuvunja mikataba yao pia maana itakuwa haina miguu ya kusimamia,” anasema.
Anasema ndiyo maana ibara ndogo ya 4 inalinda mikataba midogo na kwamba kama mikataba midogo haijapata dosari, basi IGA isivunjwe, kuahirishwa, wala kusitishwa katika mazingira yoyote.
Je, ni kweli kwamba Tanzania hawezi kutaifisha mali za mwekezaji?
Mbossa anasema ibara ya 14 (1) haijaeleza lolote kwamba Tanzania haina mamlaka ya kutaifisha mali za mwekezaji.
“Kilichopo ni kwamba Tanzania inamhakikishia mwekezaji na wahusika wengine katika uwekezaji kuwa haina nia ya kutaifisha mali zao.
“Katika hali ya kawaida ni vugumu kuingia kwenye biashara wakati kwenye mkataba ukamwamia mwekezaji kwamba tuna nia ya kuja kutaifisha mali zako,” anasema.
Mkataba unazuia Tanzania kutunga sheria mpya?
Anasema Ibara ya 27 haizuii Tanzania kutunga sheria mpya yoyote bali yanazuia pande za mkataba kutotunga sheria au kuingia makubaliano au mikataba ya kitaifa na kimataifa inayokinzana.
Anasema ukinzani huo unatokana na ama uingiaji au utekelezaji wa IGA na mikataba migine ya utekelezaji itakayotokana na mkataba huo.
“Kwa mfano unaingia mkataba na DPW ukimruhusu, pamoja na mambo mengine aendeleze bandari kavu baadae unasaini mkataba wa kimataifa unaopiga marufuku uendeshaji wa bandari za nchi kavu.
“Tayari mkataba huo wa kimataifa utakuwa unakinzana na mkataba wako na DPW kwa kuwa utamfanya ashidwe kuendesha biashara yake. Sheria au mikataba ya aina hii ndio inayozuiwa kutugwa au kuingiwa na wahusika wa IGA.
“Kitu ambacho ni sahihi kabisa. Hata katika biashara za kawaida huwezi kumkodishia mtu gari, kwa mwaka mzima, ukiwa umeisajiri kama gari ya abiria halafu miezi miwili au mitatu baada ya kumkodishia ukaenda kubadili usajiri wake kuwa gari ya mizigo,” anasema. |
Hatua ya Taasisi ya Times Higher Education (THE), kutaja orodha ya Vyuo Vikuu bora Kusini mwa Jangwa | Hatua ya Taasisi ya Times Higher Education (THE), kutaja orodha ya Vyuo Vikuu bora Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa mwaka 2023, imewagusa wadau, baadhi wakitilia shaka vigezo vilivyotumika.
Orodha hiyo iliyotangazwa na taasisi ya THE kutoka Uingereza, imekitaja Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS) kuwa nafasi ya pili, huku Chuo Kikuu cha Ardhi kikiwa nafasi ya 10.
Mbali na vyuo hivyo viwili kutoka Tanzania kuchomoza katika orodha ya 10 bora, vingine maarufu kama Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) havikuwepo kabisa katika orodha hiyo.
Hata hivyo, 10 bora ya orodha hiyo ilivihusisha vyuo vya Makerere kutoka Uganda kilichoshika nafasi ya tano na UGHE cha Rwanda kikishika nafasi ya nane.
Orodha ya vyuo vikuu bora kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara iliyozinduliwa Juni 26, mwaka huu, ni utaratibu mpya kutolewa na THE, ikilenga kubaini na kukabiliana na changamoto zinazozikabili taasisi hizo.
Taratibu zilizohusika katika kutaja orodha hiyo ni miongoni mwa sababu zilizokifanya Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) kisishiriki, licha ya kutajwa mara kadhaa kuwa moja ya taasisi bora za elimu ya juu, kama anavyofafanua Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Raphael Chibunda.
"Hatukutuma maombi katika shindano hilo kwa sababu inakubidi ulipie, inaonekana kama biashara na hata hivyo, unaweza kutuona katika orodha mbalimbali ikiwemo webometrics ndiyo maana vyuo vingi maarufu havimo kwenye orodha,” alisema.
Mbali na Profesa Chibunda, wadau wengine walibainisha changamoto na kutoeleweka kwa utaratibu uliotumika kupanga orodha hiyo, hali waliyosema imetoa mwanya kwa vingine kufanya janjajanja.
"Kwa ujumla huu ni mkakati wa kutangaza unaolenga kuviingiza vyuo katika orodha ya dunia. Hatuwezi kusema vyote vilivyopo kwenye orodha hiyo ni bora kiasi hicho.
"Kama chuo kinataka kujitangaza kimataifa, hii ni moja ya njia ya kuvutia wanafunzi wengi. Lakini orodha hii haipaswi kupimwa kama ndiyo ubora,” alisema Dk Thomas Jabir, mshauri wa elimu kutoka Dar es Salaam.
Mhadhiri wa zamani wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Dk Eugenia Njovu alisema orodha hiyo ni sehemu ya kuimarisha ubora wa taasisi hizo, kwa kuwa kila kimoja kitahitaji kuwa na vigezo stahiki ili kitajwe.
"Nimeshtuka kuona vyuo vikubwa vya Afrika Mashariki kama Nairobi, Kenyatta na SUA havipo kwenye orodha, hii inaibua maswali mengi,” aliongeza.
Kaimu Makamu Mkuu wa MUHAS, Profesa Appolinary Kamuhabwa alisema uwekezaji katika tafiti zinazogusa jamii na uzalishaji wa wataalamu bora katika sekta ya afya wanaotoa huduma ndani na nje ya nchi ndiyo siri ya mafanikio.
"Tumefanya kazi nyingi za utafiti na sasa tunatafuta wawezeshaji katika miradi zaidi ya 135 inayolenga kukidhi mahitaji ya jamii… watafiti wamechapisha katika majarida maarufu.
"Tunaboresha kwa kuongeza program muhimu ili kuendelea kuandaa wataalamu bora katika sekta ya afya, tukiamini kwamba siku moja tutaongoza hilo ndilo lengo letu,” alisema.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Profesa Evaristo Liwa alisema mbinu zinazotumika katika ufundishaji na kuwapa wanafunzi ujuzi shindani ndicho kigezo walichotuma kwa THE na kupata nafasi hiyo.
"Wanafunzi wetu wamezisaidia Manispaa nyingi katika masuala ya ardhi. Hii ni kwa sababu tunajihusisha nao mara nyingi kusaidia masuala hayo katika Manispaa,” alisema. |
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali itafanyika kazi maoni na ushauri wote unaotolewa na wa | Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali itafanyika kazi maoni na ushauri wote unaotolewa na wananchi kuhusu sakata la uwekezaji bandari kati yake na Dubai.
Kauli ya Majaliwa, ameitoa kujibu wito wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), ulioitaka Serikali kupokea maoni ya wananchi na kufafanua vifungu vinavyowatia mashaka.
"Nitoe wito kwa Serikali kupokea maoni ya wananchi na kufafanua maeneo yote yanayotiliwa mashaka," alisema Mruma alipohutubia Baraza la Eid El-Adh'ha katika Msikiti wa Mohammed wa VI jijini hapa.
Hata hivyo, hii ni kauli nyingine ya Majaliwa, baada ya ile aliyoitoa siku tisa zilizopita akiahidi Serikali haitapuuza maoni wala ushauri wa wananchi kuhusu sakata hilo.
Msingi wa mjadala kuhusu bandari ni dosari zilizopo katika mkataba wa awali kati ya Tanzania na Dubai (IGA), unaotajwa kuathiri maslahi ya taifa.
Kwa mujibu wa wadau mbalimbali kikiwemo Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), baadhi ya vifungu vina mkanganyiko wa kisheria na kuiweka rehani bandari.
Hata hivyo, tayari bunge Julai 10 mwaka huu lilisharidhia kupitishwa kwa mkataba huo.
Akizungumza katika baraza hilo jana, Majaliwa alisema kilichopitishwa na bunge ni makubaliano ya ushirikiano baina ya Tanzania na Dubai.
"Kilichofanyika kwanza ni kuanza kutengeneza makubaliano yanayoweka misingi kwenye eneo husika.
"Kwa hiyo, Tanzania imekubaliana kuwa na mahusiano kwenye eneo la uwekezaji wa Bandari na Dubai na ndilo azimio lililopelekwa bungeni kuridhiwa," alisema.
Baada ya makubaliano hayo, alisema yatafuatia makubaliano kuhusu maeneo ambayo DP World inapaswa kufanyia kazi na hapo ndipo Serikali itakapozingatia maoni ya wananchi.
"Kwenye maeneo ya uwekezaji hapo sasa ndipo tutazingatia maoni yenu, lakini hatuchukii mkishauri, mkitoa maoni ni jambo zuri," alisema.
Hata hivyo, Majaliwa alieleza kinachofanywa na DP World si kuchukua bandari, bali itapewa baadhi ya maeneo kwa ajili ya kufanya kazi yake.
Alieleza umiliki wa bandari utaendelea kusalia kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa mujibu wa sheria.
"Tunachokifanya ni kama ilivyokuwa kwa TICTS atapewa maeneo ya kufanyia kazi na atafanya hayo," alieleza.
Kuhusu hofu ya usalama, alieleza kama TICTS imekuwepo kwa miaka 22 bila kuathiri ulinzi na usalama wa nchi, itawezekanaje DP World iupoteze.
Alisema kinachofanywa na Serikali ni kuhakikisha inatumia rasilimali za ndani kuonya uchumi na katika hilo itazingatia maslahi ya taifa.
"Tunasikia maoni, ushauri na hofu zote lakini nataka niwaambie tunayafanyia kazi kwa lengo lile lile la kuhakikisha tunaweka mbele maslahi ya taifa," alisema.
Kwa sababu bandari ina washindani wengi, alisema Serikali imeona haja ya kufanya maboresho mbalimbali ili kuwa na ushindani.
Changamoto kubwa iliyopo katika bandari hiyo, alieleza ni ufanisi licha ya uwekezaji uliofanywa na Serikali.
Nyingine aliyoitaja ni kuchelewa kwa upakuaji na upakiaji mizigo katika meli.
Akihutubia katika ibada ya sikukuu hiyo, Kaimu Sheikh wa Dar es Salaam, Walid Omar alisisitiza umuhimu wa waislamu kufuata matakwa ya Mungu kama ilivyoamrishwa katika kitabu chake cha Quran.
"Hii si sikukuu ya kusherehekea tu, bali tukumbuke kumcha Mwenyezi Mungu kama alivyoamrisha," amesema.
Mbali na Majaliwa, wengine waliokuwepo katika ibada hiyo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, Naibu
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila alitaka amani katika kusherehekea siku hiyo. |
Mjadala wa ukomo wa muda wa utumishi wa Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma umeibua dosari k | Mjadala wa ukomo wa muda wa utumishi wa Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma umeibua dosari katika Katiba, baada ya kile kilichoelezwa na wadau kuwa, vifungu vilivyopo katika Katiba ya sasa vinaleta mkanganyiko wa kisheria juu ya suala hilo.
Chimbuko la mjadala huo ni taarifa kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan amemuongezea muda Profesa Juma wa kuendelea kuwa Jaji Mkuu, jambo lililopingwa na wadau wa sheria, akiwemo Jaji wa Mahakama ya Rufani, Stella Mugasha.
Kutokana na uamuzi huo wa Rais Samia, Jaji Stella anadaiwa kuandika barua kueleza kilichofanywa ni uvunjaji wa Katiba na kutozingatia misingi ya sheria, akiielekeza kwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Profesa Elisante Ole Gabriel na viongozi wengine wa Serikali.
Msingi wa hoja ya Jaji Stella ni matakwa ya Katiba ya Tanzania, Ibara ya 120 (1) inayosema: “Kila Jaji wa Mahakama ya Rufani atalazimika kuacha kazi yake atakapotimiza umri wa miaka 65, lakini masharti ya ibara hii ndogo yatatumika bila kuathiri masharti yafuatayo katika ibara hii”.
Hata hivyo, uamuzi wa Rais Samia ni kwa mujibu wa Ibara ya 120 (3) ya Katiba ya Tanzania, inayompa mamlaka mkuu wa nchi kumwongezea muda Jaji wa Mahakama ya Rufani hata akifikisha muda wa kustaafu, iwapo ataona kuna manufaa ya umma.
Kulingana na Ibara hiyo, “Iwapo Rais ataona kuwa kwa ajili ya manufaa ya Umma inafaa Jaji wa Mahakama ya Rufani aliyetimiza umri wa miaka 65 aendelee kufanya kazi na huyo Jaji mwenyewe wa Mahakama ya Rufani anakubali kwa maandishi kuendelea kufanya kazi.
“Basi Rais aweza kuagiza kuwa Jaji huyo wa Mahakama ya Rufani aendelee kufanya kazi kwa muda wowote utakaotajwa na Rais.”
Maelezo ya vifungu hivyo, ndipo unakoanzia mkanganyiko ulioibua dosari katika Katiba kwa mujibu wa wataalamu wa sheria wakiwemo waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali katika sekta hiyo.
Mkanganyiko katika Katiba
Akizungumzia hilo, Jaji Mstaafu Amir Manento alisema ni vugumu kuweka wazi kwamba uamuzi wa kuongezewa muda kwa Jaji Mkuu ni kosa au si kosa.
Hiyo ni kwa sababu ya kile alichoeleza kuwa, Katiba ya Tanzania imetaja miaka 65 kama muda wa kiongozi huyo kustaafu, lakini kwa upande mwingine imetoa mwanya wa kuongezewa muda.
Hatua hiyo, kwa mujibu wa Jaji Manento ndiyo inayosababisha mkanganyiko.
“Mkanganyiko zaidi ni pale ambapo Katiba yenyewe haijaeleza kwamba muda huo anaoongezewa Jaji Mkuu ni nyongeza ya muda wa kustaafu au anaongezwa kwa mkataba?” alisema.
Kwa muktadha huo, Manento ambaye ni Mwenyekiti wa zamani wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, alionyesha haja ya marekebisho ya Katiba ili kuondoa mkanganyiko uliopo.
“Haiwezekani Katiba hiyo hiyo inatoa muda wa kustaafu na hiyo hiyo inampa mamlaka Rais kuongeza muda wa kustaafu tena bila kufafanua nyongeza hiyo ya muda ni ya mkataba au vipi,” alieleza.
Alijitolea mfano wakati wa utumishi wake, alipofika umri wa miaka 60 alistaafu lakini aliongezewa muda kwa mkataba katika wadhifa wa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.
“Huwezi kusema Rais kakosea kwa sababu amepewa mamlaka hiyo na Katiba, lakini Katiba yenyewe ndiyo yenye changamoto haijafafanua kutosheleza,” alisema.
Kuhusu kilichofanywa na Jaji Stella, mkongwe huyo katika mihimili ya sheria, alisema ni kizuri na muhimu kwa kuwa kinawaamsha wenye mamlaka ya mabadiliko ya kisheria kuona kasoro zilizopo.
Hata hivyo, alibainisha mkanganyiko kama huo si mara ya kwanza kutokea, iliwahi kufanyika hivyo na kwamba kuna umuhimu wa mabadiliko ili utaratibu ueleweke.
Hoja ya Jaji Manento inaungwa mkono na Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Leonard Shaid aliyesema Katiba haijaweka sawa jambo hilo.
“Kilichoelezwa na Katiba ni kwamba Rais anaweza kumuongezea muda Jaji wa Mahakama ya Rufani, lakini haikumtaja Jaji Mkuu, hapa ndipo mkanganyiko ulipo,” alisema.
Alieleza kulingana na Katiba hiyo, Jaji wa Mahakama ya Rufani anaweza kuongezewa muda akifikisha miaka 65, lakini haikuelezwa chochote kwamba nyongeza hiyo itamfanya kuendelea kuwa Jaji Mkuu.
Lakini, alisema namna nzuri na bora ya uongozi katika wadhifa huo, ni kustaafu iwapo utafikisha umri wa miaka 65 na kwa kuwa wengine wapo wateuliwe kuongoza.
“Kama Jaji Mkuu Mstaafu, Chande Othman yeye alipomaliza muda wake alistaafu na alionyesha wazi kwamba hakuwa na nia ya kuendelea hata angeongezewa muda,” alisema.
Lissu: Rais amevunja Katiba
Akizungumzia hilo, Mtaalamu wa Sheria, Tundu Lissu alisema kulingana na Katiba Jaji Mkuu hawezi kuongezewa muda, wanaoruhusiwa kufanyiwa hivyo ni Jaji wa Mahakama Kuu na wale wa Mahakama ya Rufani.
“Msimamo huu umewekwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) tangu mwaka 2007 na haujabadilishwa hadi leo. Na uliwekwa hivyo kutokana na mabadiliko ya mwisho ya Katiba ya sasa yaliyofanyika mwaka 2005,” alisema.
Katika ufafanuzi wake, Lissu alisema mabadiliko hayo ya mwaka 2005 yalilenga kuondoa mkanganyiko uliotokea wakati Jaji Mkuu wa wakati huo, Francis Nyalali akiongezewa muda mara mbili baada ya kustaafu.
“Ilionekana kwamba, bila kubadilisha Katiba, tunaweza kuwa na Jaji Mkuu wa maisha, kitu ambacho kinakatazwa na Katiba yetu,” alisema.
Alisisitiza kuwa kilichofanywa na Rais Samia ni ukiukwaji wa Katiba, lakini alisema ipo nafasi ya mkuu huyo wa nchi kujirekebisha kwa kufuta nyongeza hiyo ya muda na kumteuwa mwingine anayestahidi wadhifa huo.
“Kwa Katiba yetu, Jaji Mkuu hana ulinzi wa kikatiba wa nafasi yake hiyo, bali ana ulinzi wa nafasi yake kama Jaji wa Rufaa tu. Kwa hiyo, kwa Rais Samia kufuta hiyo nyongeza haramu ya muda, hatakuwa amevunja ulinzi wa kikatiba wa utumishi wa Jaji Mkuu,” alisema Lissu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Bara.
Alipoulizwa kuhusu hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk Eliezer Feleshi alikiri kuwa na taarifa ya barua iliyoelekezwa kwake kuhusu hilo, lakini atapata cha kuzungumza baada ya kuisoma. |
Kukosekana ushirikishwaji wa wananchi, mlolongo mrefu wa utatuzi wa migogoro na ukinzani wa kisheria | Kukosekana ushirikishwaji wa wananchi, mlolongo mrefu wa utatuzi wa migogoro na ukinzani wa kisheria ni miongoni mwa kasoro zilizotajwa kugubika mkataba wa ushirikiano katika uwekezaji na uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai.
Msingi wa kasoro zote hizo zilizotajwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), ni kile ilichoeleza kuwa Serikali haikutoa nafasi kwa wananchi na wadau kushiriki mchakato wa kupendekeza, kujadili na kuamua kuhusu mkataba huo.
Hoja hizo zimetolewa na timu ya wataalamu wa sheria iliyoundwa na TLS baada ya kuibuka kwa mitazamo tofauti kutokana na uamuzi wa Serikali kusaini mkataba huo wa awali (IGA) na Serikali ya Dubai kupitia kampuni ya DP World.
Timu hiyo ya wataalamu ya TLS iliongozwa na Makamu Mwenyekiti wa TLS, Aisha Sinda, akisaidiwa na Dk Hawa Sinare, huku wajumbe wengine wakiwa ni mawakili Mpale Mpoki, Stephen Mwakibolwa na Mackphason Mshana.
Hata hivyo, timu hiyo iliyopewa siku 14 kutekeleza majukumu ya uchambuzi na Juni 12 ilitakiwa kukabidhi ripoti yake, jambo ambalo halikukamilika kwa wakati na hatimaye taarifa hiyo ilitolewa juzi.
Katika uchambuzi huo, uliotolewa juzi na TLS, Serikali ilitakiwa kutengeneza utaratibu wa kuwashirikisha wananchi katika hatua za upangaji, majadiliano na uamuzi juu ya masuala yote yanayohusu rasilimali za nchi.
Kulingana na taarifa hiyo, kufanya hivyo ni takwa la kikatiba Ibara ya 21 inayoeleza kila mwananchi ana uhuru na haki ya kushiriki kikamilifu katika mchakato utakaosababisha uamuzi utakaomuathiri yeye au ustawi wa taifa.
Kasoro
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mchakato wa Bunge kuuridhia mkataba huo ni mfupi kiasi cha kukosekana muda wa kutosha wa wananchi kutoa maoni.
TLS ilisema Serikali ilialika wananchi Juni 6 kwa ajili ya Juni 7 mwaka huu kwenda kutoa maoni yao bungeni, muda ambao ulikuwa mdogo kufanikisha hilo.
“Tunaitaka Serikali na bunge kuheshimu matakwa ya kikanuni na kisheria inayohusu ushirikishwaji wa wadau,” ilieleza taarifa hiyo.
Hata hivyo, chama hicho kilipendekeza maboresho ya utaratibu wa kuridhia mikataba ya kimataifa, kadhalika kanuni ya kudumu ya bunge ya mwaka 2020, kifungu cha 18 ili kuimarisha jukumu la muhimili huo katika uidhinishaji.
“TLS inaomba Kanuni za Kudumu zifanyiwe marekebisho kutoa muda wa kutosha kwa wadau kuchambua kwa kina mikataba na kuwasilisha mapendekezo yao kwa Kamati za Bunge zinazohusika,” ilieleza.
Kasoro nyingine iliyobainishwa na TLS ni katika ibara ya 20 ya IGA, inayotaka migogoro baina ya pande mbili kutatuliwa kwa njia ya usuluhishi, huku kukiwa na mlolongo wa siku lukuki zinazopaswa kufanikisha mchakato huo.
“Muda kabla ya kufanya ombi la usuluhishi ni mrefu zaidi (Siku 90). Kuna haja ya kuupunguza, kipindi cha makubaliano hakipaswi kuzidi muda wa siku 90,” ilieleza taarifa hiyo ya TLS.
Utata mwingine wa mkataba huo kwa mujibu wa TLS ni katika kifungu cha 21, kinachotaka sheria za Kiingereza kusimamia na kuongoza makubaliano hayo.
Katika hilo, TLS ilisema ni kawaida kuwepo mikataba inayosimamiwa na sheria zisizo za Tanzania lakini si masuala ya haki ya ardhi, uwekezaji, mazingira na ulinzi na usalama.
Kwa muktadha huo, chama hicho kilipendekeza kupitiwa upya kwa ibara hiyo na kutoa nafasi kwa sheria za Tanzania kusimamia mkataba huo.
Kulingana na TLS, ibara ya 23 (1) ya mkataba huo inaainisha dhana mbili za kusitishwa kwake, ambazo ni kusitisha shughuli zote za mradi na ile ya kuisha kwa mkataba wa miradi yote ya makubaliano (HGA).
Aidha, TLS inasema kifungu cha 23(2) kinaeleza nafasi ya kurefushwa mkataba unaopaswa kusitishwa kwa makubaliano ya pande mbili ili kuwezesha upande mmoja kudai haki zake.
Pamoja na hayo, kifungu cha 23(3) kinasema mkataba huo utasitishwa kwa ridhaa ya upande mwingine na haupaswi kuzuiwa bila sababu.
“Ibara ya 23(4) inatamka kuwa nchi wanachama haziruhusiwi kushutumu, kujiondoa, kusimamisha au kusitisha mkataba huu katika hali yoyote,” ilieleza.
Katika hayo TLS ilipendekeza, kufutwa kwa vifungu 23(3) na 23(4) vya mkataba huo, huku ikisisitiza vifungu 23(1) na 23(2), ni muhimu kuhifadhiwa.
Pendekezo lake la kufutwa kwa vifungu hivyo, linatokana na kile akilichoelezwa na taarifa hiyo kuwa, vinaminya nafasi ya upande wowote wa nchi zilizokubaliana kuvunja mkataba hata ikitokea hali inayoathiri maslahi ya nchi.
Kulingana na TLS, ibara ya 25 (1) inailazimisha Tanzania kutekeleza kiutawala na hatua za udhibiti baada ya kusaini mkataba ili kuhakikisha shughuli za awali zinaendeshwa kisheria kwa niaba ya mwekezaji mmoja au zaidi au kampuni ya mradi.
Katika kifungu hicho, TLS inapendekeza kuondoa marejeleo yote ya mradi wa awali kutoka mkataba wa IGA. TLS inachukulia kuwa kuna hati iliyopo ya kisheria inayosimamia shughuli za mradi wa mapema, ambazo zinapaswa kutosha kama sheria iliyojitegemea.
Katika hatua nyingine, chama hicho kilibainisha ahueni na fursa ya Serikali kufanya marekebisho ya kasoro zote zinazolalamikiwa na umma kupitia ibara ya 22 ya mkataba huo.
Kwa mujibu wa TLS, ibara hiyo inaeleza marekebisho ya mkataba huo yanaweza kufanywa wakati wowote kwa maandishi kupitia makubaliano ya pande za nchi husika.
“Zaidi ya hayo, inabainisha hakuna marekebisho yatakayofanyika bila makubaliano, yaliyoainishwa kwa saini na kuridhiwa na/au kupitishwa kwa nyaraka na nchi zilizokubaliana,” inaeleza TLS.
Kuhusu hilo, TLS inapendekeza kwa kuwa kuna mapungufu lukuki yanayozungumzwa na wananchi na wadau katika mkataba huo, Serikali inapaswa kuitumia ibara hiyo kuyashughulikia. |
Swali la nani atakayekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, baada ya Profesa Ibrahim Juma ndilo linalogonga vic | Swali la nani atakayekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, baada ya Profesa Ibrahim Juma ndilo linalogonga vichwa vya wengi kwa sasa.
Kuibuka kwa swali hilo nyakati hizi, kunatokana na mkuu huyo wa muhimili wa mahakama, kufikisha umri wa miaka 65 wiki iliyopita, ambao kwa mujibu wa Katiba uongozi wake unapaswa kukoma.
Ibara ya 120(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, inasema kila Jaji wa Mahakama ya Rufani atalazimika kuacha kazi yake atakapotimiza umri wa miaka 65.
Lakini, upo mwanya wa mkuu huyo wa mahakama kuendelea na wadhifa huo kwa matakwa ya Rais, kama inavyofafanua Ibara ya 120 (3) ya katiba hiyo.
“Iwapo Rais ataona kuwa kwa ajili ya manufaa ya umma inafaa Jaji wa Mahakama ya Rufani aliyetimiza umri wa miaka 65 aendelee kufanya kazi na mwenyewe anakubali kwa maandishi kuendelea kufanya kazi.
“Basi Rais anaweza kuagiza kuwa Jaji huyo wa Mahakama ya Rufani aendelee kufanya kazi kwa muda wowote utakaotajwa na Rais,” inaeleza ibara ya 120 (3) ya katiba hiyo.
Halitakuwa jambo jipya kwa Profesa Juma kuendelea kuongoza muhimili huo, licha ya umri wake kutia nanga, iliwahi kutokea kwa Jaji Mstaafu Barnabas Samatta aliyeongezewa miaka miwili na Rais Jakaya Kikwete wa wakati huo na kustaafu mwaka 2007 akiwa na umri wa miaka 67.
Swali la ukomo au kusalia kwa Profesa Juma katika wadhifa huo, linapata mkanganyiko zaidi kutokana na hatua iliyochukuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan Mei 18, mwaka huu ya kuteuwa Majaji sita wa Mahakama ya Rufani.
Kulingana na Katiba, Jaji Mkuu kwa maneno mengine anatambulika kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Hivyo, hisia za wengi ni kwamba uteuzi wa anayefuata kushika wadhifa huo, atatokea katika moja ya majaji wa mahakama ya rufani wateule wa hivi karibuni na hasa wengine wanahoji atakuwa wa jinsi gani?
Mtazamo wa wanasheria
Akizunguma na Mwananchi, mtaalamu wa sheria na mwanzilishi mwenza wa Timu ya Wanasheria wa Mazingira (LEAT) Dk Rugemeleza Nshala, alisema Katiba haijaweka ukomo wa muda ambao Jaji Mkuu ataongezewa baada ya kufikisha umri wa kustaafu.
"Katiba imetaja tu kwamba kwa matakwa ya Rais Jaji wa Mahakama ya Rufani ataendelea kushika wadhifa huo hata baada ya kufikisha umri wa kustaafu,” alisema.
Hata hivyo, Dk Nshalla alisema hadhani kwamba Profesa Juma ataongezewa muda, akirejea historia za majaji kadhaa waliomtangulia, walistaafu wakiwa na miaka 65.
Aliwataja Majaji hao ni Othman Chande aliyezaliwa mwaka 1952 na kustaafu mwaka 2017 akiwa na umri wa miaka 65, kadhalika aliyemtangulia Hayati Jaji Augustino Ramadhani aliyezaliwa 1945 na kustaafu 2010 akiwa na miaka 65.
Vuguvugu la kupatikana kwa Jaji Mkuu mwanamke linaibuliwa na Mtaalamu mwingine wa sheria na mwanaharakati wa haki za binadamu, Dk Helen Kijo Bisimba.
Pamoja na Rais Samia kuongoza muhimili wa Serikali na Dk Tulia Ackson kuongoza wa Bunge, uamuzi wa kumteuwa Jaji Mkuu mwanamke kuuongoza muhimili wa Mahakama itakuwa hatua kubwa.
"Atakuwa Jaji Mkuu wa kwanza wa kike na kuna idadi kubwa ya wanawake waliopo katika mahakama ya rufaa ambao wana sifa na uwezo wa kushikilia wadhifa huo," alisema.
Iwapo utafanyika uteuzi wa jinsia hiyo, kwa mujibu wa Dk Bisimba, Tanzania itadhihirisha dhamira yake ya kukuza ushirikishwaji na fursa sawa kwa wote.
Huyu ndiye Profesa Juma
Aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na Rais Jakaya Kikwete mwaka 2008 kabla ya kupandishwa cheo na kuitumikia Mahakama ya Rufani mwaka 2012.
Pia, aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Sheria Tanzania (LRCT).
Kabla ya kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu mwaka 2008 na Rais Kikwete, Profesa Juma alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Akiwa UDSM aliwahi kuwa Mkuu wa Kitivo cha Sheria kabla ya kuukwaa wadhifa wa Jaji wa Mahakama Kuu. |
Juzi nilimsikia mmoja wa wasomi wabobevu wa masuala ya Sayansi ya Siasa na utawala wa umma kutoka Ch | Juzi nilimsikia mmoja wa wasomi wabobevu wa masuala ya Sayansi ya Siasa na utawala wa umma kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Rwekaza Mukandara akieleza kuhusu mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa nchi za Afrika.
Katika maelezo yake, Profesa Mukandara alitaja takwimu zinazoonyesha karibu robo ya nchi hizo zinavita vya wenyewe kwa wenyewe au ndani yake kuna vikundi vya waasi.
Haya yanatokea kipindi ambacho karibu nchi zote 54 za Afrika zimeshavuka muongo mmoja tangu zianze kujitawala, maana Namibia ndiyo nchi ya mwisho kupata uhuru mwaka 1990.
Kwa nadharia ni kweli nchi za Afrika zimepata uhuru kwa sababu zinaamua zenyewe kuhusu nani atakayeziongoza kwa muda gani, ingawa ndani ya michakato ya kufanikisha hayo kuna malalamiko lukuki.
Tukiingia kwenye demokrasia ndani ya nchi za Afrika, huo ni mjadala mwingine mpana kwani karibu nchi zote barani hapa hakuna aliyeshindwa uchaguzi akakubali kushindwa kihalali.
Hii maana yake, kulikuwepo na mazingira yanayomfanya ashuku mchakato wa kuwapata viongozi, hayo ni matundu katika Demokrasia yanapaswa yazibwe.
Sitaki kujikita katika changamoto za demokrasia ndani ya mataifa husika, nitaeleza mtazamo wangu kuhusu vita vya wenyewe kwa wenyewe katika baadhi ya nchi za Afrika, kwamba chanzo ni ndani au yupo wa nje mwenye maslahi navyo?
Katika kipindi hiki cha miongo kadhaa baada ya uhuru, bado zimeshuhudiwa nchi za Afrika zikishikiana mitutu ama migogoro ya ndani au nchi moja na nyingine.
Licha ya miaka mingi kupita bado ndani ya Bara hili lililotakiwa kuungana na kutengeneza umoja kama walivyotaka waasisi wake, linakabiliwa na vikundi vya waasi ambao kila kukicha vinachafua amani iliyopo.
Nakubali kwamba uhuru wa nchi si uhakika wa usalama wake, lakini matarajio ya uhuru ni kuimarika kwa usalama na amani kwa kila Taifa.
Hata wakati wa harakati za uhuru wa mataifa mengi barani hapa, shabaha ilikuwa kujitawala ili kuwa na amani na usalama, lakini kuwa na uwezo wa kujiamria wenyewe.
Pamoja na matunda ya kuwa na uchaguzi tunaojisimamia wenyewe, lakini bado Afrika imeendelea kutawaliwa katika baadhi ya maeneo hasa nyeti.
Bado nchi nyingi za Afrika hazina nguvu ya kujisimamia katika matumizi na mgawanyo wa rasilimali zake, mara nyingi hii ndiyo sababu ya migogoro ya ndani.
Mafanikio ya uhuru wa nchi za Afrika, hayakuziwezesha kutengeneza mifumo imara ya kutawala rasilimali zake na kufanya mgawanyo utakaomtosheleza kila mwananchi.
Kilichobaki kila mmoja anahisi kudhulumiwa, aghalabu kinachoaminika sehemu kubwa ya rasilimali hizo zinaliwa na walizopewa nafasi ya kuwawakilisha wananchi.
Hasira ya kunyonywa ndiyo inasababiHa fukuto la chuko na hatimaye wananchi wanajenga uadui na viongozi na ndipo vita vya wenyewe kwa wenyewe vinapoanza.
Lakini kwa upande mwingine, kukosekana kwa mifumo imara ndani ya Serikali itakayowezesha mgawanyo wa rasilimali hizo, ndiyo sababu unapatikana mwanya kwa mataifa ya nje kuingilia rasilimali hizo.
Imeshuhudiwa katika mataifa mengi, nchi za Ulaya zikitia mguu na kuneemeka na rasilimali za mataifa ya Afrika ilhali nchi husika zinabaki na ufukara.
Uhuru tuliojipatia haukutengeneza misingi ya kusimamia, kuziendeleza na kunufaika na rasilimali zetu, badala yake tulijenga misingi ya kujitawala kwa kumpata Rais mweusi aliyezaliwa katika taifa husika.
Uhakika wa amani katika taifa la Afrika, utatokana na umasikini wake wa rasilimali, lakini mara nyingi nchi zenye utajiri wa rasilimali zinakosa amani wakati wote.
Hapa ndipo hoja ya nchi za Afrika zinapigana au zinapiganishwa inapoanzia.
Libya ni moja ya mifano halisi ya nchi za Afrika ambazo amani yake imeponzwa na utajiri wa rasilimali zake.
Kwa sasa taifa hilo limebaki kuwa mtaji wa nchi za nje ya Afrika, zinazojichotea mafuta, ambayo ndiyo yaliyokuwa yanaipa jeuri nchi hiyo kiuchumi.
Waliotaka kuiunganisha Afrika, walilenga kuifanya kuwa Bara litakalojitegemea kiuchumi na mambo mengine muhimu kwa maslahi ya usalama wake.
Kama hilo lingetokea, leo hii isingeyalazimu mataifa ya Afrika kusaka sekta binafsi au wawekezaji kutoka nje kwa ajili ya kusaidia uendeshaji au uboreshaji wa rasilimali za ndani yake.
Kungeshakuwa na teknolojia za uendelezaji, mifumo ya uboreshaji wa rasilimali zilizopo na hatimaye zingetumika na kuwanufaisha wa Afrika. |
Mfumo mbaya wa mgawanyo wa rasilimali, matumizi mabaya ya mipaka ya nchi na maslahi ya mataifa ya nj | Mfumo mbaya wa mgawanyo wa rasilimali, matumizi mabaya ya mipaka ya nchi na maslahi ya mataifa ya nje ni miongoni mwa sababu zilizotajwa kuwa kiini cha migogoro ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi za Afrika.
Sababu hizo zinatajwa na wanazuoni wakati karibu robo ya mataifa 54 ya Afrika yanakabiliwa na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe na mengine kuna makundi ya waasi ndani yake.
Si hivyo, kauli hizo zinakuja kipindi ambacho nchi saba za Afrika zinaongozwa na Jeshi, hivyo hazifuati tena utawala wa demokrasia kama ilivyohitajika na waasisi, kadhalika zipo zile ambazo wakuu wake hawang’atuki madarakani.
Sababu na suluhu ya migogoro hiyo, zilibainishwa jijini Dar es Salaam jana, katika mkutano wa 14 wa kidoda cha Mwalimu Julius Nyerere uliozungumzia, Umajumui wa Afrika, katika Demokrasia, Ulinzi na Maendeleo.
Akizungumza katika mkutano huo, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, Profesa Musambayi Katumanga alisema hatua ya nchi za Afrika kutokubaliana kuungana tangu mwanzo ndiyo sababu ya kushindwa kutatua migogoro yake yenyewe.
Lakini, Mtaalamu huyo wa Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma, alisema mgawanyo wa mali ni kiini cha kwanza cha migogoro miongoni mwa nchi hizo.
“Hakuna mfumo mzuri wa mgawanyo wa rasilimali katika nchi za Afrika, hii inasababisha wengine wadhulumiwe au kuona wanadhulumiwa na hapo ndipo migogoro huanza.
“Serikali hazijatilia maanani kuweka kuimarisha utamaduni utakaowezesha kuwapatia wananchi rasilimali vema,” alisema.
Mipaka ya nchi ni kiini kingine cha migogoro ya wenyewe kwa wenyewe kilichotajwa na Profesa Katumanga akisema iliwekwa na wakoloni kwa sababu za kiutawala.
“Walioweka mipaka ya nchi na nchi ni watu wengine na walifanya hivyo kwa sababu zao, mataifa yanapigana kwa sababu ya kukosa umoja,” alisema.
Kuanzishwa kwa sera za pamoja zitakazohakikisha rasilimali zinazozalishwa zinatumika ndani ya bara husika ni moja ya suluhu muhimu.
“Sera za pamoja zianzishwe kuhakikisha kwamba rasilimali ambazo Serikali hazina uwezo wa kuziendeleza zinaendelezwa kwa pamoja na zinatumika na wananchi,” alisema.
Akizungumzia hilo, Profesa wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere cha Umajumui wa Afrika kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Rwekaza Mukandara alisema ugomvi katika mataifa ya Afrika kwa sehemu kubwa unachagizwa na maslahi ya nchi za nje.
“Afrika inapaswa kukaa kimkakati kuhakikisha inadhibiti na kujenga uwezo wa kutambua matatizo yake yenyewe na kutatua migogoro yake yenyewe, isiingiliwe na taifa linguine,” alisema.
Mwenyekiti wa Bodi ya Hakielimu, Rochard Mabala alisema ingawa umajumui unaendelea kufundishwa sasa, ni muhimu vijana waeleweshwe ili wauelewe na wanavyonufaika nao.
“Tunapoongelea umajumui, vijana wetu wanajua, inawahusu kiasi gani, wamesikilizwa kujua wanautafsirije?” alihoji.
Kwa kuwa mkutano huo unazungumzia masuala ya demokrasia, alieleza hata elimu inapaswa kutolewa kwa kufuata misingi hiyo na kuendana na mabadiliko ya ulimwengu. |
Si ushamba, lakini ndivyo uhalisia ulivyo kwamba ni kiu ya wengi kuishi maghorofani na aghalabu anay | Si ushamba, lakini ndivyo uhalisia ulivyo kwamba ni kiu ya wengi kuishi maghorofani na aghalabu anayeishi kwenye nyumba za namna hiyo, hutafsiriwa kuwa na uwezo kiuchumi.
Maisha katika nyumba hizo, si rahisi kushuhudia wapangaji wakizozana hadharani au familia moja kuwa na uhuru wa kuingia kwenye eneo la mwingine kupiga soga, kila mtu huishi kivyake.
Pamoja na hewa safi inayopatikana kutokana na kuishi mita kadhaa kutoka usawa wa ardhi, maisha ya ghorofani hutazamwa kuwa tofauti na nyumba nyingine za kawaida, lakini hali ni tofauti katika maghorofa ya Magomeni Kota.
Kwa namna yalivyo majengo hayo, ubora na mvuto wa mwonekano wake, itakushangaza ukipata angalau saa 72 za kushuhudia vituko, visa na vimbwenga vya maisha ya wakazi wake.
Achana na lugha chafu zinazotamkwa kwa sauti kubwa na watu wazima katika majengo hayo, burudani rahisi kusikika Magomeni Kota si muziki, ni ugomvi unaohusisha kurushiana maneno kati ya mkazi mmoja na mwingine.
Mwandishi wa Gazeti hili aliyeishi katika eneo hilo, anasimulia visa na vituko vya wakazi wa Magomeni Kota anavyovishuhudia.
Ugomvi, matusi
Si ajabu kusikia au kumuona mtu mwenye rika la mzazi, akitoa lugha chafu dhidi ya mwingine tena kwa sauti ya juu.
Hiyo inafanyika bila aibu na wakati mwingine mbele ya watoto.
Zilivyojengwa nyumba hizo, zimewekewa mazingira yanayolazimu kila mtu kuishi kivyake, lakini hilo limewashinda baadhi ya wakazi wa eneo hilo.
Utashangaa pamoja na mazingira hayo, haichukui wiki kushuhudia wakazi wakigombana, hasa hugombea vitu ambavyo kila mmoja anamiliki cha kwake.
Hazipiti siku tatu katika eneo hilo, bila kushuhudia ama ugomvi wa kupigana kati ya mtu mmoja na mwingine, au kurushiana maneno machafu.
Umbea, mapenzi na kulazimisha kujua maisha ya wengine, ndiyo sababu kubwa za ugomvi kwa wakazi hao kama inavyoelezwa na Mama Aisha mkazi wa eneo hilo.
“Kinachowagombanisha watu ni mapenzi ugomvi mara nyingi unasababishwa na mambo ya wivu, watu wanaibiana wanaume wengine wanaibiana wanawake.
“Kuna wale watu wazima wakimuona binti kavaa mavazi fulani wanadhani anawatega wenza wao, ugomvi huwa unaanzia hapo,” anasema.
Hata hivyo, ugomvi ndiyo burudani pendwa miongoni mwa wakazi wa eneo hilo, kwani unapotokea wengi huchomoza vichwa madirishani kushuhudia na wengine hukimbilia eneo la tukio.
Usitarajie suluhu ya haraka inapotokea wakazi wanagombana, aghalabu wengine huketi pembeni kuona kinachoendelea, huku baadhi wakichochea kwa maneno na wakati mwingine kujikuta sehemu ya ugomvi kama anavyoeleza Asnat Keko mkazi wa Magomeni Kota.
“Hapa mwenzangu ukilianzisha usitarajie utapata msaada, kama huna uwezo wa kuongea au hauna nguvu tulia, maana watu watakuona unagombana wanachungulia madirishani.
“Kuna mtu amewahi kupiga kelele watu waliishia kuchungulia dirishaji hakuna aliyetoka kwenda kushuhudia kinachofanyika,” anasema Asnat.
Katika mazingira hayo, hakuna anayechuja neno la kuzungumza. Ataongea kila linalotoka mdomoni kwa sauti inayowezesha wakazi wa ghorofa zima kusikia.
Wizi
Kwa namna makazi hayo yalivyoboreshwa, ilitarajiwa kusiwepo baadhi ya tabia zinazodhalilisha utu wa mtu ikiwemo wizi na udokozi hasa wa vitu vidogo.
Unapoishi Magomeni Kota usithubutu kuanika nguo ukaiacha hadi asubuhi, hutaikuta. Wengi huamua kujimilikisha vya watu bila woga.
Kibaya zaidi, nguo iliyoibwa leo kesho inavaliwa hadharani na ikifuliwa inaanikwa bila kificho, kama una uwezo wa kutukana na kugombana kutwa nzima kathubutu kuidai.
“Hapa udokozi ndiyo umetawala. Watu wanaibiana nguo na vitu vidogo vidogo hata kijiko ukiacha vibaya wanabeba, huna pa kwenda anakwambia vijiko vinafanana au nguo zinafanana.
“Hupati la kusema kwa sababu kweli vitu vinafanana lakini chako utakijua tu, kwa kuepusha ugomvi inabidi unyamaze,” anaeleza Marian Mushi mkazi wa eneo hilo.
Hao ni wachache kati ya wengi wanaoiba nguo na usizione tena, hali hiyo inawafanya wengi kufua na kuanika nguo mpya ndani.
Hayo yanafanyika si kwamba hakuna ulinzi au waliopo hawana weledi, hapana. Kwa namna palivyo walinzi hukaa getini kudhibiti uhalifu kutoka nje, kumbe wa ndani wenyewe kwa wenyewe ndiyo mkubwa zaidi.
Si mavazi pekee, kama unataka kupunga upepo kwa kuacha madirisha wazi, maisha ya Magomeni Kota yatakushinda, wapo wanapenya madirishani kujichukulia vya ndani bila woga, Simon Nyere anafafanua.
“Watu wanaiba hadi vitu vya ndani kama hutakuwa makini, ndiyo maana hata ukienda jikoni unashauriwa ufunge mlango, kwa kuwa hapa kuna watu wengi na kila mmoja ana tabia zake,” anasema.
Vituko vingine
Hamtapata usingizi wa raha iwapo itatokea siku timu kubwa kati ya Simba au Yanga zimecheza, huo utakuwa usiku wa shangwe, kuzomeana, kelele na watu wakizunguka huku na kule kiasi ya kuweka mazingira magumu ya kulala.
Katika hilo, Nyere anasema kama ilivyo kwenye maeneo mengine mpira wa miguu ni mchezo wenye washabiki wengi, hivyo ikitokea ushindi wa timu yoyote kati ya hizo mbili watu hushangilia.
“Kibaya ni namna wanavyoshangilia, wanazunguka hadi maghorofani wanapiga matarumbeta hata usiku mzito bila kujali kwamba kuna waliolala au laa,” anasema.
Usitarajie kila unaposalimia utajibiwa kuna wakati hutajibiwa na wakati mwingine huyo huyo atalalamika kwanini humsalimii.
Vicheko baada ya kupita, nyimbo za taarabu, watu wazima kunengua mbele ya hadhara ni mambo mengine yaliyogubika maisha ya Magomeni Kota.
Utofauti wa maisha na malezi inatajwa kuwa sababu ya aina hiyo ya maisha kwa wakazi hao, kama inavyofafanuliwa na Neema Mtemi mmoja wa wakazi wa eneo hilo.
Kabla ya kuishi eneo hilo, alisema kila mmoja aliishi kwingineko, wamekutanishwa na hivyo kila mtu anaonyesha tabia alizotokanazo alikotoka.
“Hawa watu waliwahi kuishi pamoja, baada ya nyumba kuvunjwa wakatenganishwa kila mmoja ameiga tabia zake huko alikokuwa, wamerudi na kuwekwa pamoja kila mmoja anaonyesha tabia yake mpya,” anasema.
Nichorous Tweve anayeishi eneo hilo, alisema kati ya wakazi wote hakuna aliyetarajia kuishi kwenye nyumba zenye hadhi hiyo.
Wakati mwingine, anasema wanajisahau na kuendeleza tabia za uswahilini ilhali wapo kwenye eneo lisilotaka mtindo huo wa maisha.
“Mtu haamini kama anaishi kwenye maghorofa haya na mazuri yana kila kitu ndani. Wanaishi kama walivyokuwa wakiishi zamani na kuna wengine hawana amani, wanatamani wazurure lakini hapa hakuna hilo,” anaeleza.
Kinachofanywa nao, kinatajwa kuchagizwa na ugeni wao katika aina hiyo ya makazi kama inavyofafanuliwa na Katibu wa wakazi katika moja ya majengo ya eneo hilo.
Ushirikiano kwenye misiba
Mbali na vituko vilivyopo, katika nyumba hizo unapotokea msiba kila mkazi anawajibika kuchangia sehemu ya fedha isiyopungua Sh1,000 kwa ajili ya salamu za rambirambi.
“Mtu mmoja anatakiwa kutoa Sh1,000 kama mwanakota kwa ajili ya rambirambi unapotokea msiba, hasa wale wanaokaa kwenye jengo ambalo msiba umetokea huwa wanatakiwa kulipa wote,” anasema Mariam Dadi mkazi wa eneo hilo.
Anaeleza kiasi hicho cha fedha hutumika kuwafariji wafiwa, kadhalika kugharimia sehemu ya mahitaji muhimu katika shughuli ya mazishi.
Mwenyekiti
Mwenyekiti wa Wakazi hao, George Abel anasema changamoto zinazoshuhudiwa sasa zinasababishwa na wananchi kukosa uzoefu na mazingira yaliyopo sasa.
Kulingana na Abel, kabla ya maghorofa hayo miaka zaidi ya 10 iliyopita wananchi hao waliishi maeneo hayo kwenye nyumba ndogondogo za chini na kutoka nyumba moja hadi kuifikia nyingine ilikuwa safari ndefu.
“Hili eneo lina ekari 35 kwa hiyo tulivyokuwa tunaishi zamani kutoka nyumba moja hadi nyingine inakuchukua muda mrefu, lakini kwa sasa zimejengwa nyumba za kisasa, pia zipo jirani eneo la ekari kama nne au tano,” anasema.
Ukaribu wao, anautaja kuwa chanzo cha vituko wanavyovifanya na hata hivyo, Abel anaeleza kwa sasa vinapungua kwa kadri siku zinavyokwenda.
Kwa mujibu wa Abel, eneo hilo la ekari tano lina takriban kaya 3,000 hivyo na kwa kuwa hazijazoea maisha ya nyumba hizo ndiyo maana wanaishi tofauti na uhalisia.
“Mwanzo kabisa ndiyo kulikuwa na matatizo mengi, ugeni ule uliwafanya watoto wachezee mara lifti yaani kila kitu ilikuwa shida, mimi naona kadri siku zinavyokwenda wanabadilika na naamini utafika wakati watu watabadilika kabisa,” anasema.
Ingawa hakubainisha idadi ya kesi za ugomvi na wizi anazopokea kwa siku, Mwenyekiti huyo anasema amekuwa akizipokea na kuzisuluhisha kwa njia ya mazungumzo.
“Kwenye watu wengi hili ni jambo la kawaida, wamekuwa wakija mara kwa mara lakini ni ule ugomvi wa kawaida tunatatua unakwisha, kesho wanakuja wengine hivyo hivyo,” anasema. |
Tulikuwa tunahesabu mwaka na sasa imebaki miezi sita kabla ya kuanza utekelezaji wa rasimu ya sera y | Tulikuwa tunahesabu mwaka na sasa imebaki miezi sita kabla ya kuanza utekelezaji wa rasimu ya sera ya elimu na mitalaa, ambayo kimsingi imekuja na mabadiliko makubwa katika sekta hiyo.
Sera na mitalaa hiyo kwa mujibu wa Kamati iliyoshiriki kukusanya maoni, inatarajiwa kuanza kutekelezwa katika mwaka wa masomo 2024, kwa maana Januari mwakani.
Ndani ya sera na mitalaa hiyo, kuna mabadiliko makubwa ya sekta ya elimu yanayohitaji uwekezaji unaolingana na tunachokitarajia kutoka katika sera na mitalaa hiyo.
Kwa sababu ya ukubwa wa kinachotarajiwa, ni muhimu Serikali ikaeleza sasa juu ya ilipofikia katika maandalizi ya utekelezaji wa nyenzo hizo zinazotazamwa kama msingi wa Mageuzi ya elimu Tanzania.
Kwa sababu hatma ya malalamiko dhidi ya sekta ya elimu itatokana na utekelezwaji mzuri wa sera hiyo, taarifa ya hatua iliyofikiwa juu ya maandalizi ya utekelezaji wake isiwe siri.
Kila mmoja anatambua kwamba Serikali unafanya maandalizi ya utekelezaji huo, lakini ni kitu ya wengi kutambua kiwango cha maandalizi kilichofikiwa.
Katika sera na mitalaa hiyo, kuna hitaji la aina mpya ya walimu ambayo haikuwa kipaumbele zaidi nchini, hawa ni wale wa elimu ya ufundi stadi.
Kabla ya mabadiliko haya, Tanzania ilijikita katika uzalishaji wa walimu wa ufundi stadi kulingana na mahitaji machache ya Vyuo vya ufundi stadi vilivyokuwepo nchini.
Ingawa Serikali ilijizatiti na kuweka wazi mpango wake wa kujenga vyuo hivyo katika kila halmashauri, bado uzalishaji wa wataalamu watakaotumika kufundisha katika taasisi hizo haukutosheleza.
Kama hawakutosheleza katika vyuo vya ufundi stadi napata mashaka tutawapata wapi wa haraka kuwapeleka shuleni, bila kuathiri nguvukazi inayohitajika katika vyuo vya ufundi stadi.
Ufundi stadi ni jambo moja, yapo maeneo mengine lukuki kama lugha ya Kiarabu, Kichina na Kifaransa.
Masomo haya yote yanahitaji idadi ya walimu itakayokidhi mahitaji, najiuliza Serikali itawaajiri wote kwa mkupuo? Na je, tukiwahitaji kwa sasa wanapatikana?
Hayo ni mambo mapya katika sera na mitalaa hiyo, lakini yapo yale yaliyokuwepo yanahitaji maboresho ya umahiri wa wataalamu wetu.
Mathalan, kuna mfumo mpya wa ufundishaji unaolenga si kujenga umahiri pekee, bali kumuandaa mwanafunzi asiwe tegemezi atakapohitimu elimu ya lazima.
Hii maana yake ni kwamba mwanafunzi atakayehitimu kidato cha nne, awe na uwezo wa kubuni na kufanya shughuli itakayomuwezesha kujiingizia kipato, lakini kutengeneza fursa za ajira.
Hili halihitaji maandalizi ya umahiri wa walimu pekee, bali ni mabadiliko ya fikra na mitazamo ya wafundishaji na wafundishwaji wenyewe.
Kwa sababu ni muda mrefu tumejikita katika kumfundisha mwanafunzi awe na uwezo wa kusoma, kuandika lakini umahiri darasani, bila shaka mabadiliko haya wapo watakaoyaona mzigo kwao.
Ili kuendana nayo ni vema Serikali ianze sasa kubadili mitazamo ya walimu, wanafunzi na wadau wengine katika mnyororo wa thamani wa elimu, ili ieleweke na kila mmoja kuhusu mabadiliko tarajiwa.
Mabadiliko ya fikra hizi hayatafikiwa kwa kuwasimulia wadau hao kuhusu mitalaa na sera mpya, bali wapigwe msasa darasani, jambo ambalo linahitaji uwezeshaji kifedha.
Kwa sababu ya matarajio chanya waliyonayo baadhi ya wadau na hasi kutoka kwa wengine, angalau utekelezwaji wa sera na mitalaa hii uanze kwa angalau asilimia 70.
Tukianza chini ya hapo haitakuwa rahisi kuyaona matunda yake, jambo litakaloibua kelele zile zile zinazosikika sasa kuhusu sekta ya elimu.
Wakati haya yanafanyika na kwa sababu matumaini makubwa ya ufanisi katika mabadiliko hayo tunayaacha kwa Mwalimu, Serikali itafute namna ya kuwapa motisha.
Mwalimu asibaki kupondwa anapokosea bali anapofanya vema apewe motisha itakayompa nguvu ya kuongeza ubunifu katika ufundishaji.
Tusiache eneo la malalamiko kwa wadau hawa muhimu walioshika hatma ya elimu yetu, tuhakikishe tunawatosheleza kwa mahitaji.
Hayo yaende sambamba na miundombinu ya ufundishaji, kama ni Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, basi mitambo isimikwe sasa.
Wataalamu wafundishwe namna ya kuitumia kiasi cha kueleweka na wanafunzi. |
Zikiwa zimebaki siku mbili kwa Serikali kupitisha bajeti yake ya mwaka wa fedha 2023/24, chama cha C | Zikiwa zimebaki siku mbili kwa Serikali kupitisha bajeti yake ya mwaka wa fedha 2023/24, chama cha Chadema kimesema kilichowasilishwa katika mapendekezo kinawapa matumaini hewa wananchi.
Kauli yake hiyo inatokana na kile ilichokifafanua kuwa, uzoefu unaonyesha malengo ya makusanyo kulingana na bajeti za kila mwaka hayakuwahi kufikiwa, hivyo ni vigumu kilichopangwa kutekelezwa.
Chadema inakuja na kauli hiyo, zikiwa zimesalia siku mbili kabla ya Serikali kuwasilisha bungeni jijini Dodoma bajeti kamili baada ya kujadiliwa tangu Juni 15, mwaka huu ilipowasilishwa.
Hata hivyo, chama hicho cha upinzani kimependekeza kupunguzwa malengo katika bajeti hiyo, kikisisitiza yawekwe kulingana na uwezo wa nchi kukusanya.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika alisema katika bajeti ya mwaka wa fedha unaokaribia kuisha 2022/23 asilimia 21.9 ya makusanyo hayakukusanywa.
“Jambo hili linaibua swali kuwa kama Serikali imeshindwa kufikia malengo ya makusanyo ya Sh41.48 trilioni katika bajeti yam waka wa fedha 2022/23, itawezaje kukusanya kufikia malengo ya kukusanya Sh44 trilioni inayopendekezwa,” alihoji.
Hata hivyo, Mtendaji Mkuu huyo wa Chadema alisema bajeti hiyo haikulenga kuwapa unafuu wa maisha wananchi, badala yake imejikita katika kulipa madeni, mishahara na matumizi ya kawaida.
Kauli yake hiyo inathibitishwa na uchambuzi wa bajeti uliofanywa na chama hicho, unaobainisha asilimia 60.4 ya matumizi yameelekezwa kwenye kulipa madeni ya nyuma, mishahara ya watumishi na matumizi ya kawaida.
Kulingana na Mnyika, ni asilimia 29.6 pekee ndiyo imeelekezwa kwenye maendeleo ambayo pia, pengine isikamilike kwa kuwa kilicholengwa hakitakusanywa chote.
“Kwa kiwango kikubwa bajeti hiyo ni ya kulipana mishahara, matumizi ya kawaida na kulipa madeni badala ya kuleta maendeleo ya wananchi,” alisema Mnyika.
Alisema chama hicho kilitarajia bajeti hiyo ingejibu tatizo la kupotea kwa makusanyo kati ya asilimia 20 hadi 30 kulingana na ripoti mbalimbali za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Ukuaji uchumi
Alishuku matumaini ya ukuaji wa uchumi wa asilimia nane kwa mujibu wa mpango wa maendeleo endelevu na asilimia 10 kulingana na dira ya maendeleo ya taifa.
Mnyika alisema imebaki miaka miwili kukamilisha dira ya maendeleo inayotaka ukuaji wa uchumi uwe asilimia 10 kila mwaka lakini hadi sasa ukuaji ni chini ya lengo hilo.
Mwaka 2022/21, alisema uchumi ulishuka na kufikia asilimia 4.8, kutoka asilimia saba ya mwaka 2019/20.
Hata hivyo, Mnyika alisema pamoja na changamoto ya kupanda kwa bei ya bidhaa na gharama za maisha, lakini bado Serikali kupitia bajeti hiyo haijaonyesha mikakati ya kuleta ahueni.
Hilo linatokana na kile alichoeleza kuwa, kupitia bajeti hiyo Serikali imependekeza tozo na ushuru katika bidhaa muhimu jambo ambalo litaongeza gharama za maisha.
Miongoni mwa tozo hizo ni Sh100 kwenye mafuta ya petroli, itakayoongeza gharama za maisha kwa kuwa bidhaa hiyo ni muhimu katika kila sekta.
"Wakati wananchi wanalalamikia ugumu wa maisha, Serikali hii umeamua kupeleka bungeni muswada wa sheria wa kuwaongezea gharama za maisha," alisema.
Eneo lingine aliloeleza linaongeza ukali wa maisha ni mabadiliko pendekezwa ya sheria ya forodha ya Afrika Mashariki yanayotaka kutozwa ushuru wa asilimia 25 kwenye matairi ya pikipiki kutoka nje.
“Serikali inaweka ushuru huu wakati haina viwanda vya kuzalisha matairi nchini kiasi cha kukidhi haja ya pikipiki zilizopo,” alisema.
Maeneo mengine aliyoeleza ni ongezeko la kodi ya majengo, ushuru katika kila kilo moja ya saruji na ongezeko la asilimia 50 katika miaka ya kutoa fedha.
Kama inataka kurekebisha madhara ya tozo za miamala ya simu, irudishe utaratibu wa miaka ya 2021 ya kuondoa tozo zote ili kuondoa mzigo kwa walaji wa mwisho.
Katiba Mpya
Mnyika alisema pamoja Serikali kuridhia kuanza mchakato wa Katiba Mpya, katika bajeti hiyo haikuweka wazi kiwango cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya mchakato huo.
"Tulitarajia hotuba ya bajeti ya Serikali ingeeleza kiwango cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya mchakato wa Katiba Mpya, lakini haikuelezwa," alisema.
Mnyika alisema awali taarifa kuhusu mchakato huo ilielezwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro ambaye pia hakueleza kiwango cha fedha kilichotengwa.
Hata hivyo, Mtendaji Mkuu huyo wa Chadema alisema taarifa za ndani walizonazo ni kwamba kati ya Sh5 bilioni hadi Sh9 bilioni zimetengwa.
Mbaya zaidi, alieleza kiwango hicho walichoarifiwa kumetengwa si kwa ajili ya kufungua mchakato huo, bali ni kuwaelimisha wananchi kuhusu Katiba ya mwaka 1977.
Wakati Mnyika anaeleza hayo, Serikali imetenga Sh5 bilioni kwa ajili ya kugharimia mchakato huo.
Katika mjadala wa bajeti hiyo, Juni 22, mwaka huu, Mbunge wa Nkasi (Chadema) Aida Kenani aliitaka Serikali iharakishe utoaji wa fedha hiyo.
Hoja za Chadema zinapigiwa msumari na mchumi kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine mkoani Morogoro (SUA), Charles Malaki aliyesema kinachochagiza makusanyo yasifikie matarajio ni kukosekana mfumo mpya.
Alipendekeza kuanzishwa mfumo mpya utakaowainua waliopo kwenye sekta isiyo rasmi hatimaye warasimishwe na kuwa chanzo cha mapato.
Kwa mujibu wa Malaki, hilo litawezekana iwapo Serikali itaweka kipaumbele kugharimia sekta inayogusa wananchi wengi.
“Serikali iamue kuweka fedha nyingi kwenye sekta moja au kadhaa zinazowagusa wananchi kwa mfano kilimo, ili kuhakikisha inawainua wakulima hadi wanafikia hatua ya kuwa walipa kodi,” alisema.
Kwa kinachonyika sasa, alieleza itakuwa vigumu kufikiwa kwa malengo ya makusanyo kwa kuwa hata fedha inayopelekwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli, wakati mwingine haifiki hata asilimia 10.
“Ziangaliwe njia mbadala za kukuza uchumi, kama kuwekeza asilimia 10 ya pato ya taifa kwenye sekta inayogusa watu wengi na hasa sekta isiyolipa kodi ili kuongeza vyanzo vya mapato.
“Kama tunatoa fedha mbele ya macho ya watu lakini uhalisia tunapeleka asilimia tisa hatutafika,” alisema. |
auli ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwamba Serikali haitapuuza maoni ya wananchi kuhusu Mkataba wa | auli ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwamba Serikali haitapuuza maoni ya wananchi kuhusu Mkataba wa Ushirikiano wa Uendeshaji na Uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam, imewaibua wadau wakitaka utekelezaji wa vitendo.
Hii ni kauli ya kwanza ya Serikali mbali na zile za kujibu mapigo ilizozitoa kutokana na ukosoaji mkubwa kutoka kwa wananchi juu ya mkataba huo uliosainiwa kati yake na DP World ya Dubai.
Kulingana na wadau hao, pamoja na kauli hiyo ya Majaliwa kuwa ya matumaini, hayatafikiwa iwapo hakutakuwa na utekelezaji wa kilichoelezwa.
Majaliwa alitoa kauli hiyo juzi, jijini Arusha, alipohutubia katika sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya Chuo cha International Evangelism Centre.
“Serikali haitodharau maoni na ushauri wanaoutoa kuhusu maeneo yenye hofu kwenye mradi wa uwekezaji wa Bandari ya Dar es Salaam.
“Endeleeni kuwa na imani na Serikali na wawakilishi wake ndani ya Bunge, kwani imejizatiti kuhakikisha bandari inakuwa na ufanisi unaoendana na mahitaji ya sasa,” alisema Majaliwa.
Kauli ya Majaliwa inakuja wiki tatu sasa, tangu kuwepo kwa ukosoaji mkubwa kutoka kwa makundi mbalimbali ya wananchi kuhusu mkataba huo.
Malalamiko dhidi ya mkataba huo pamoja na mambo mengine yanahusu kifungu cha 23 kinachoeleza kuwa Serikali husika katika mkataba huo, hazitakuwa na haki ya kuuvunja, kujitoa, kuahirisha au kusitisha katika mazingira yoyote.
Ukomo wa muda wa mkataba huo ni jambo lingine linaloibua mzozo miongoni mwa Watanzania kiasi cha baadhi kueleza kuwa, kuingia mkataba huo ni sawa na kuiuza nchi.
Hasira zaidi ya wananchi ilishuhudiwa baada ya Juni 10, mwaka huu bunge liliporidhia kuendelea kwa mkataba huo.
Hata hivyo, sakata la mkataba huo halikuishia kuwa na wakosoaji pekee, wapo waliounga mkono, likiwemo Shirika la kubadili maisha ya Wanawake na Vijana nchini (Tafeyoco), kupitia tamko lao la juzi.
Msingi wa hoja yao ya kuunga mkono inatokana na kile lilichokieleza kupitia taarifa hiyo kuwa, uwekezaji huo utaimarisha ufanisi wa bandari na hatimaye kuongeza mapato ya nchi.
“Kuna kipindi cha miaka mingi tu kuna Kampuni ya wazawa ilipewa kazi pale bandarini lakini malalamiko ya wateja na utendaji na uzalishaji mdogo wa mapato hadi Serikali ikaamua kuiondoa.
“Hao watu wapo mitaani kwetu lakini walishindwa kuiendesha TICTS vizuri kwa faida ya nchi na Serikali hadi wakaondolewa,” iliongeza sehemu ya taarifa hiyo.
Wadau kuhusu kauli ya Majaliwa
Akizungumzia kauli ya Majaliwa jana, Mtaalamu wa Sheria, Dk Rugelemeza Nshalla alisema namna pekee ambayo Serikali inapaswa kufanya ili kuthibitisha kuwa haidharau maoni ya wananchi, ni kuvunja mkataba huo.
Haja ya kuvunjwa kwake, alisema inatokana na mchakato wa mkataba husika na wote kwa ujumla haukufuata Katiba ya nchi.
“Kama hautodharau maoni au ushauri wa wananchi, basi inapaswa kufuata Katiba, kwa sababu mkataba unakiuka Katiba uondolewe au waanze upya mchakato,” alisema.
Kulingana na Dk Nshalla, mkataba huo ulipaswa kuanza na mjadala wa kitaifa utakaohusisha wananchi waeleze wanavyotaka bandari zao ziendeshwe.
“Bandari ni mali ya wananchi, lazima uwashirikishe wenye mali yao waeleze wanataka iendeshwe vipi, ndivyo Katiba inataka,” alifafanua.
Akisisitizia hoja hiyo, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga alisema kilichoelezwa na Serikali hakipaswi kubaki mdomoni, utekelezaji unapaswa kuonekana.
Alipendekeza namna ya kuyatekeleza maneno hayo, ni kupitia kifungu cha 22 cha mkataba huo kinachotoa mwanya kwa Serikali ya Tanzania kuiandikia DP World ombi la kusitisha utekelezaji kwa muda.
“Serikali inapaswa kuiomba DP World kwa maandishi kwamba wananchi ambao ndiyo wenye mali yao, wamepata mkanganyiko kwa hiyo tusitishe utekelezaji kwanza hadi hapo tutakapowasikiliza wananchi wanachohitaji,” alisema.
Ni kauli ya matumaini
Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema alisema pamoja na kauli hiyo kuwa ya matumaini, hayatafikiwa iwapo hakutakuwa na utekelezaji wa kilichoelezwa na Waziri Mkuu.
Kulingana na Lema, ni imani yake kwamba kilichozungumzwa hakilengi kupooza joto lililopo, bali Serikali itazingatia mapitio upya ya mkataba huo.
“Kauli hiyo itakuwa ya maana zaidi kama Serikali itazingatia kinachoshauriwa, kimsingi ni wajibu wa Serikali kusikiliza wananchi kwa kuwa ndiyo wenye nchi na yenyewe inawajibika kwao,” alisema.
Katika utekelezwaji wa maoni ya wananchi, mwanasiasa huyo alishauri yasitafsiriwe kwamba yalilenga kuibeza Serikali, bali ifarijike kwa kuwa na taifa lenye wananchi wanaojali rasilimali zao.
Alisisitiza kuwa Serikali inapaswa kujua kwamba ni wajibu wake kuwasikiliza wananchi kwa sababu inafanya kazi kwa niaba yao.
“Pamoja na yote, wasitoe mamlaka yote ya bandari kwa yeyote sio tu mgeni hata kwa mzawa, wahakikishe sheria zinakuwa za msingi kulinda rasilimali za nchi hasa vitu sensitive ambavyo ukifanya makosa ya kisheria utajuta baadaye na hivi ndivyo vitu vinavyoleta hasira na kusababisha watu wasielewane,” alisema.
Lakini kwa upande mwingine, alisema ni aibu kwa Bunge ambalo ndilo lililopaswa kutoa maoni ya kuonyesha mashaka na mkataba husika, badala yake wajibu wake umetekelezwa na wananchi.
“Leo hii tulipaswa kumsikia Waziri Mkuu akisema hatutapuuza maoni ya wabunge, lakini wameshindwa kuona mambo hayo na wananchi wamechukua nafasi yao na kulalamika.
“Bunge maana yake ni wananchi ndani ya bunge, lakini wabunge hawakuona, hii ni hatari kwamba hatuna bunge linaloona,” alisema.
Kutokana na kauli hiyo ya Waziri Mkuu, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoriki Tanzania (TEC), Charles Kitima alisema ni imani yao kuwa Serikali itarekebisha vifungu vinavyolalamikiwa katika mkataba huo.
“Tuna imani Serikali itarekebisha vifungu ambavyo wananchi wamepigia kelele viko bayana,” alisema.
Kulingana na Kitima, anatarajia mwekezaji huyo (DP World) atapewa sehemu ya yule aliyeondoka, akimaanisha TICTS, kadhalika Serikali kupitia TPA iingie ubia na mwekezaji kwa kila mradi.
Pamoja na hayo, Dk Kitima alitaka malalamiko dhidi ya rushwa na maslahi binafsi yafanyiwe kazi baada ya vifungu kushughulikiwa. |
Huenda bidhaa ya maji, ikawa miongoni mwa zitakazopanda bei, iwapo bajeti ya Serikali ya mwaka wa fe | Huenda bidhaa ya maji, ikawa miongoni mwa zitakazopanda bei, iwapo bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/24 itapitishwa.
Matarajio ya ongezeko la bei katika bidhaa hiyo, yanatokana na hatua iliyopendekezwa na Serikali ya kuongeza ushuru maalum wa asilimia 10 katika bidhaa zisizo za petroli zinazohusisha maji.
Hata hivyo, hatua hiyo imelalamikiwa na Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI), wakisema kiwango pendekezwa hakilingani na bei halisi ya bidhaa husika, ikilinganishwa na nyingine kwenye kundi hilo kama soda.
Nyongeza ya ushuru wa asilimia 10 katika bidhaa hiyo, ilipendekezwa na Serikali kupitia bajeti yake yam waka wa fedha 2023/24 iliyowasilishwa bungeni jijini Dodoma Juni 15, mwaka huu na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba.
Akiwasilisha hoja hiyo ndani ya bajeti Dk Nchemba alisema: “napendekeza kufanya marekebisho ya viwango maalum vya ushuru kwa kiwango cha asilimia 10 ya bei kwenye bidhaa zisizo za petroli na asilimia 20 ya bei kwenye bidhaa za bia na tumbaku,” alisema.
Hata hivyo, pendekezo la nyongeza hiyo litafanya lita moja ya maji itozwe ushuru wa Sh75.2 badala ya Sh58 unaotozwa sasa, ambayo hata hivyo ilikuwa ikilalamikiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uchambuzi wa bajeti hiyo, Makamu Mwenyekiti wa CTI, Hussein Sufiani alisema umefika wakati Serikali iangalie upya ushuru unaotozwa katika maji.
Alisema nyongeza hiyo ya ushuru katika bidhaa ya maji imekuja kipindi ambacho hata iliyopo sasa ya Sh58 kwa lita inalalamikiwa.
“Tangu mwaka 2012 tumekuwa tukiomba punguzo katika ushuru wa bidhaa hiyo, tulipendekeza iwe nusu ya Sh58 hii ni kutokana na umuhimu wa bidhaa husika,” alisema.
Hata hivyo, Sufiani alisema katika bidhaa zote zilizojumuishwa kwenye ushuru huo, ikiwemo soda hakuna hata moja yenye bei inayofanana na lita moja ya maji.
Alieleza lita moja ya maji inayouzwa Sh500 inahusisha gharama nyingine lukuki kama usafirishaji na mambo mengine hivyo ushuru huo utaongeza gharama.
“Wanachama walipeleka ombi kutokana na mwenendo wa biashara walifikiri mabadiliko yoyote yangekuwa na athari kwenye kiwango cha mauzo kwa sababu yatasababisha ongezeko la bei,” alisema.
Kwa hali ilivyo, alisema ni wakati wa Serikali kuangalia upya ushuru maalum katika bidhaa ya maji ya kunywa ili kuleta unafuu kwa wazalishaji.
Pamoja na kupongeza baadhi ya marekebisho katika bajeti hiyo, Sufiani alisema yapo maeneo ambayo Serikali inapaswa kuzingatia ili kurahisisha zaidi mazingira ya biashara nchini.
Aliyataja maeneo mengine ni ushuru wa Sh20 uliopendekezwa kutozwa kwenye kila kilo moja ya saruji.
"Tumepata maoni kutoka kwa wazalishaji wanahisi itachangia kuongeza gharama ya uzalishaji na gharama ya bidhaa, itaathiri upatikanaji, tunaomba Serikali kulifikiria jambo hili," alisema.
Alilitaja eneo lingine ni hatua ya kupunguza ushuru wa asilimia 50 hadi asilimia 35 katika vitenge vinavyoingizwa kutoka nje, akisema itawaathiri wazalishaji wa ndani.
"Katika nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wenzetu bidhaa hii inatozwa asilimia 50 ya ushuru kwa wanaoingiza kutoka nje, basi tunapaswa tufanye hivyo ili kuwapa nafasi wazalishaji wa ndani," amesema.
Kulingana na Sufiani, eneo lingine ni kuendeleza kutoza ushuru wa asilimia 10 kwa mwaka kwenye nyuzi za pamba badala ya asilimia 25 ilivyopendekezwa kwa mujibu wa bajeti hiyo.
"Kuanzisha kodi ya ongezeko la faida kwa asilimia 10 katika mapato yanayotokana na uuzaji wa bidhaa za hewa ukaa," alisema.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa CTI, Leodgar Tenga alisema kinachofanywa na shirikisho hilo ni kutoa tamko kuhusu bajeti ya Serikali.
“Tumekuwa tukifanya hivi mara zote na tumekuwa tukipendekeza mara zote, lakini bajeti hii kwa sehemu kubwa imegusa maeneo tuliyopendekeza,” alisema. |
Serikali imetaka kufuatwa utaratibu wa uuzaji wa mazao yakiwemo ya chakula nje ya nchi, ikisisitiza | Serikali imetaka kufuatwa utaratibu wa uuzaji wa mazao yakiwemo ya chakula nje ya nchi, ikisisitiza haijapiga marufuku wakulima kufanya hivyo, isipokuwa wanapaswa kuzingatia sheria.
Kauli hiyo ya Serikali inakuja baada ya mkwamo wa siku kadhaa wa malori 120 yenye shehena ya mahindi Himo mkoani Kilimanjaro kuelekea Kenya, ambayo Mkuu wa Mkoa huo, Nurdin Babu alitaka yarudishe mzigo huo kuuza nchini.
Hata hivyo, Julai 13, mwaka huu akiwa mkoani Mwanza, Rais Samia Suluhu Hassan alishauri wakulima wasiuze mazao hayo nje ya nchi, badala yake waiuzie Serikali kujaza hifadhi ya ndani.
Kauli yake hiyo inatokana na kile alichoeleza kuwa, kuna viashiria vya dunia kukabiliwa na njaa kwa siku zijazo.
“Kwa sasa nchi ina akiba ya chakula tani 200,000 hadi 250,000, tuna mpango wa kumwaga fedha kununua chakula, tunataka kuwa na hifadhi ya chakula tani 500,000 kwa mwaka huu tunaouanza, hivyo msiuze mazao nje kwa kuwa Serikali itayanunua,” alisema.
Akizungumza na Mwananchi jana, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alisema Serikali haikupiga marufuku usafirishaji mazao nje ya nchi kwa biashara, bali imezuia kufanya hivyo bila kufuata utaratibu.
"Marufuku inayosemwa kwenye kusafirisha nje mazao yote ya Kilimo ikiwemo chakula ni kwa wafanyabishara wasiofuata utaratibu lakini kwa wanafuata utaratibu hakuna zuio lolote.
"Na utaratibu unaotakiwa kufuatwa, kwanza mfanyabiashara awe amesajili kampuni yake hapa nchini, awe amekata leseni ya kusafirisha mazao nje ya nchi, awe na Namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) na awe na leseni ya biashara," alisema.
Kulingana na Bashe, jambo lingine ambalo Serikali imezuia ni wafanyabiashara wanaotoka nje ya nchi na kuingia nchini kwenda kununua mazao na kuyasafirisha kwa leseni za biashara za madalali wa Tanzania.
Utaratibu huo, alisema unalenga kuongeza eneo la ukusanyaji wa kodi na kuhakikisha wanawarasimisha wauzaji wa nafaka nje.
“Tunataka wasafirishaji wa mazao nje waanze kupokea malipo kwa njia ya benki, haiwezekani tuuze mahindi moja ya nchi jirani tani 400,000 zaidi ya Sh300 bilioni halafu haionekani kwenye mfumo wa benki.
“Kwa mfanyabiashara yeyote kutoka nje ya nchi anayetaka kununua mazao nchini anapaswa kusajili kampuni kwa mujibu wa sheria au anunue kupitia kampuni za Watanzania,” alisema.
Urasimishaji wa biashara hiyo, alisema ni muhimu kwani Serikali inahitaji takwimu sahihi za mazao yanayosafirishwa nje ya nchi na kuondoa uholela uliopo.
Kuhusu yaliyotokea mkoani Kilimanjaro na kwingineko, Bashe alisema wafanyabiashara wengi hawakuwa na nyaraka sahihi ikiwemo leseni ya biashara na leseni ya kusafirisha nafaka nje.
Katika Mkoa wa Kilimanjaro, Babu aliwaambia madereva na wafanyabiashara kugeuza magari hayo na kwenda kuuza mahindi katika masoko ya ndani au ghala la taifa.
Babu alilazimika kufika katika eneo hilo na kutoa maelekezo hayo, baada ya magari hayo yenye shehena ya mahindi, yaliyozuiliwa tangu Juni 14, mwaka huu kuendelea kurundikana.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa baada ya kurundikana katika eneo hilo, wafanyabiashara husafirisha mizigo hiyo kwa njia za panya kupeleka nchini Kenya.
"Serikali inataka wafanyabiashara wafanye biashara na haikatazi watu kufanya biashara nje, lakini lazima mfuate taratibu, kwani kwa sasa hakuna mwenye kibali cha kupeleka mahindi nje ya nchi.
"Ingieni kwenye mtandao muombe vibali Julai mtaanza kuvipata, lakini kwa sasa mahindi yaliyopo hapa pelekeni Moshi, Arusha na maeneo mengine ndani ya nchi mkauze huko au kwenye ghala la taifa la kununua mahindi, mpaka tathimini ya chakula itakapokaa sawa," alisema.
Baadhi ya wafanyabiashara, akiwemo Melkiory Merero alisema mzigo wake anaupeleka Himo kwa kuwa anamiliki ghala huko.
Kuhusu hilo, Babu alisema kwa wafanyabiashara wote wenye maghala katika eneo hilo na Holili, wapeleke vibali vyao polisi ili vikaguliwe na wakashushe mzigo chini ya usimamizi.
Eliatosha Sawe ni mmoja wa madereva, alisema kuwepo katika eneo hilo pekee, wanatozwa Sh5,000 kwa siku kwa ajili ya ulinzi.
Kwingineko mkoani Songwe, wakulima wamelalamikia kushuka ghafla kwa bei ya mahindi na kwamba hakuna wateja.
Katika Mkoa huo, gunia la mahindi lenye kilo 100 liliuzwa kati ya Sh80,000 na Sh75,000 lakini tangu mwanzoni mwa wiki hii linauzwa Sh62000 na Sh56,000.
Leonard Msukwa ni mkulima mkoani humo, alisema kushuka kwa bei hiyo ni hatari kwa wakulima kwa kuwa wanaingia hasara.
"Tumaini letu kuwa hatua zitachukuliwa ili kunusuru hali ya kudorora kwa biashara ya mahindi na kutufanya tushindwe kunufaika," alisema. |
Hatimaye furaha imegeuka balaa, baada ya Serikali kuingilia kati sherehe ya harusi iliyokuwa ikifung | Hatimaye furaha imegeuka balaa, baada ya Serikali kuingilia kati sherehe ya harusi iliyokuwa ikifungwa, huku bi harusi akiwa ni mwanafunzi anayetarajia kujiunga na kidato cha tano mwaka huu.
Tukio hilo lililotokea katika Kijiji cha Mwawaza mkoani Shinyanga, kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa huo, Christine Mndeme lilifanyika kwa ruhusa ya wazazi wa binti huyo.
Katika harakati za kuchukua jiko, katikati ya sherehe zilizoambatana na vigeregere na burudani ya muziki, timu ya Mndeme inafika eneo hilo kusitisha kulikuwa kinafanyika.
Pamoja na kufika kwa viongozi hao wa Serikali, burudani ya muziki na vigeregere viliendelea kusikika, ikiashiria kuwa baadhi hawakujua kinachofanyika.
Baada ya kufika katika eneo hilo, Mndeme alionekana akipiga picha na maharusi hao na baadaye askari waliokuwepo waliwaongoza hadi kwenye gari kuwapeleka Kituo cha Polisi.
Hatua iliyofanywa na Mndeme katika tukio hilo, ni baada ya kupenyezewa taarifa za siri alipokuwa kijijini hapo kwenye kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia.
“Tukiwa katika utekelezaji wa kampeni ya huduma ya msaada wa sheria ya Mama Samia tukapata taarifa za mwanafunzi anaozeshwa na wazazi wake wameshapokea mahali siku nyingi, tukaweka mtego na kufanikiwa kuwakamata wakiwa katika harusi hiyo,” alisema Mndeme.
Akizungumzia tukio hilo jana, Mndeme aliwataka wazazi wa binti huyo kujisalimisha katika kituo cha polisi kutoa maelezo ya walichokifanya.
Kwa mujibu wa Mndeme, mwanafunzi huyo alichaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika moja ya shule za sekondari mkoani Tabora.
“Mwanafunzi huyu amehitimu katika shule ya sekondari Mwawaza mwaka jana na kuchaguliwa kuendelea na kidato cha tano mwaka huu, wazazi wake walikuwa wanataka kukatisha ndoto zake kwa kumuozesha bila ridhaa yake,” alisema.
Aliwataka wazazi na walezi wasiozeshe watoto katika umri mdogo, akisisitiza wanapaswa kuachwa watimize ndoto zao.
Mwanaharakati wa kupinga ukatili wa jinsia, Anascholastika Ndagiwe si busara mzazi kuzima ndoto za mtoto, ingawa ana maono na busara zake.
“Mzazi ana maono yake na ana baraka zake lakini pia mtoto ana maono yake na ndoto zake, hivyo wazazi wasizimishe nyota za watoto wao wawaache wafikie malengo yao na kuwasihi wazazi kuacha tamaa,” alisema.
Mwanaharakati mwingine kutoka Shirika la Paseshi, John Shija alisema inashangaza katika ulimwengu wa sasa kuwepo wazazi wanaoozesha wanafunzi. |
Wakulima 2,034 kutoka Mikoa ya Manyara, Dodoma, Morogoro na Shinyanga wamewezeshwa kitaaluma ili kuw | Wakulima 2,034 kutoka Mikoa ya Manyara, Dodoma, Morogoro na Shinyanga wamewezeshwa kitaaluma ili kuwa na uwezo wa kufanya kilimo kitakachohusisha matumizi ya zana bora na elimu ya fedha.
Mafunzo hayo yaliyotolewa na Kampuni ya EFTA na Wizara ya Kilimo, yamehusisha wakulima wanawake 527 na wanaume 1507 ili wawe na uwezo wa kulima kilimo bora.
Mbali na kujengewa uwezo kwenye maeneo hayo, kwa mujibu wa EFTA, wakulima hao pia wameelimishwa kuhusu mabadiliko ya tabianchi na kubadilishwa mtazamo kutoka kilimo cha mazoea na kuwekeza nguvu zaidi katika kile cha kisasa.
Hayo yalielezwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa EFTA, Nicomed Bohay wakati wa mafunzo ya siku moja wilayani Kahama, yakiwakutanisha wakulima na wadau wa kilimo kutoka maeneo mbalimbali.
“Tunatambua kilimo ni uti wa mgongo kwa uchumi wetu, lakini bahati mbaya wakulima wengi wanalima kilimo cha mazoea kisichokuwa na tija katika uzalishaji,” alisema.
Baada ya utafiti, alisema EFTA ilibaini ili kumkomboa mkulima kuna haja ya wadau wa sekta hiyo kuungana na Serikali kutekeleza wajibu huo.
“Tumekuja na mafunzo haya ambayo mkulima wetu atapata mbinu bora za kilimo na wakulima waliojifunza kwa sasa mtazamo wao kuhusu kilimo upo kibiashara na wanaziona fursa walizoahidi kuzitumia wapate tija,” alisema.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kahama, Timoth Ndanya, aliwataka wakulima kuhakikisha fursa hiyo ya mafunzo wanaitumia vizuri ili kujiletea tija.
“Sisi sote ni mashahidi kuwa Serikali imeweka nguvu kubwa na kutoa fedha nyingi katika Wilaya yetu ili kufanikisha miradi mbalimbali ya kilimo hapa kwetu,” alisema.
Alisema wanapojitokeza wadau kwa ajili ya kuunga mkono juhudi hizo ni vema fursa hiyo ichangamkiwe.
“Wametuletea elimu lakini hawakuja mikono mitupu wamekuja na zana mbalimbali za kilimo ambazo naambiwa wanazitoa kwa mikopo bila dhamana, nishauri tuchangamkie fursa hii,” alisema.
Wilaya hiyo, alisema imetenga ekari 2,600 kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na kwamba kinachohitajika ni kuona maeneo hayo yakilimwa misimu yote.
“Ili tufanikishe hili lazima tuwe na zana muhimu za kutuwezesha na hizi ambazo wenzetu wanakopesha ndizo zana zenyewe tuhakikishe tunakopa na kurejesha kwa wakati,” alisema.
Godwin Mubi ni mtaalamu wa zana za Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, alisema endapo wakulima hao watatumia mashine za kisasa kwa ajili ya shughuli hiyo, kilimo chao kitakuwa cha tija.
“Ziko zana nyingi sokoni na zote zinafanya kazi vizuri lakini kupitia mafunzo haya wakulima hawa sasa wanayo elimu ya aina gani ya mashine wanaweza kununua kulingana na maeneo waliyopo,” alisema. |
Itakuhitaji zaidi ya Sh50 milioni kukamilisha ujenzi wa nyumba ya vyumba viwili kitaalamu, iwapo map | Itakuhitaji zaidi ya Sh50 milioni kukamilisha ujenzi wa nyumba ya vyumba viwili kitaalamu, iwapo mapendekezo ya Serikali ya kutoza ushuru katika vifaa mbalimbali vya ujenzi yatapitishwa.
Kabla ya mapendekezo hayo , ujenzi wa nyumba ya vyumba viwili, yenye sebule choo na bafu kitaalamu, ukomo wa gharama za kuijenga ikijumuisha na vifaa haizidi Sh50 milioni au pungufu zaidi.
Ongezeko la gharama hizo za ujenzi, zinatajwa na wataalamu wa ukadiriaji majengo kuwa matokeo ya hatua ya Serikali kupendekeza ushuru katika vifaa mbalimbali vya ujenzi.
Akiwakilisha bajeti ya Serikali bungeni jijini Dodoma juzi, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba alipendekeza ushuru wa Sh20 katika kila kilo moja ya saruji.
Hiyo maana yake, kila mfuko mmoja wa bidhaa hiyo wenye kilo 50, utatozwa ushuru wa Sh1,000, jambo lililotajwa na wataalamu hao kuwa chachu ya nyongeza ya gharama za ujenzi.
Si saruji pekee, ushuru imependekezwa hata katika nondo ambao ni Dola za Marekani 250 kwa ujazo wa tani moja.
Marumaru nazo zitatozwa ushuru wa forodha wa asilimia 35 kwa kila mita moja ya mraba.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mkadiriaji Majengo, Ramadhan Madenge alisema ushuru huo uliopendependekezwa itaongeza gharama za ujenzi.
Akitolea mfano nyumba yenye mita squire 100 ya vyumba viwili, sebule, jiko na choo kwa sasa hadi inakamilika inahitaji Sh50 milioni au pungufu kwa ujenzi wa kitaalamu.
Lakini, iwapo ushuru uliopendekezwa utapitishwa, alieleza gharama hizo zitaongezeka maradufu na hivyo itazidi Sh50 milioni.
"Kwa ujumla sekta ya ujenzi itakuwa ngumu na gharama za ujenzi zitapanda hazitakuwa kama sasa," alisema.
Kuongezeka kwa gharama za ujenzi, Madenge akifafanua kutachagiza kupungua kwa idadi ya wenye uwezo wa kujenga nchini.
Si nyumba pekee, miradi ya kimkakati itaathirika kwa kuwa inahitaji vifaa vya ujenzi ikiwemo saruji ili ikamilishwe kama inavyoelezwa na Mkurugenzi kutoka Taasisi ya Huduma za Kifedha ya OASIS, Marcelino Kilyenyi.
"Hii itakwenda kuathiri na sekta nyingine, maana fedha zilizotengwa kwa ajili ya mradi fulani itabidi ziongezeke hivyo, iliyotarajiwa kutumika kwenye eneo lingine itatumika kwenye ujenzi," alisema.
Kilyenyi ambaye pia ni mshauri wa Masuala ya Kikodi, alisema hatua hiyo itaathiri Watanzania kupata makazi bora.
Ingawa Serikali imependekeza kuondoa kodi ya ongezeko la Thamani (VAT) kwenye nyumba za biashara zisizozidi gharama ya Sh50 milioni, alisema ongezeko la ushuru vifaa vya ujenzi vitafanya isipatikane nyumba ya gharama hiyo.
"Tujiulize huku tumepunguza VAT, Je, kwa kuongeza gharama za saruji, nondo na vifaa vingine havitasababisha ujenzi wa hizo nyumba tunazosema za Sh50 milioni uongezeke?" alihoji.
Alichokisema Kilyenyi, hakitofautiani na Mshauri wa Masuala ya Kikodi na Mtaalamu wa Uhasibu na Fedha kutoka, Stambuli Myovela aliyesema ushuru huo utapunguza idadi ya Watanzania watakaokuwa na makazi bora.
"Sh20 kwenye saruji bado itaumiza watu wengi na kwa kuwa sekta hiyo ndiyo inakuwa, ukiweka kodi kwenye saruji unaathiri sekta," alisema. |
‘Ni safu kuelekea michakato ya kisiasa’ ni neno fupi lililotumiwa na wataalamu wa siasa kutafsiri ut | ‘Ni safu kuelekea michakato ya kisiasa’ ni neno fupi lililotumiwa na wataalamu wa siasa kutafsiri uteuzi alioufanya Rais Samia Suluhu Hassan wa wasaidizi wake katika eneo la siasa na uhusiano na jamii.
Kauli za wasomi hao zinakuja siku moja baada ya Rais Samia kufanya uteuzi huo, uliohusisha wateule wanne katika eneo hilo, ambao ni Waziri wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Balozi Mstaafu wa Tanzania nchini Msumbiji, Rajab Luhwavi.
Wengine walioteuliwa ni Mwenyekiti mstaafu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo na Waziri wa zamani wa Nchi, Ofisi ya Rais, Huduma za Jamii na Utawala Bora visiwani Zanzibar, Haji Omar Kheir.
Mbali na uteuzi huo kutafsiriwa kuwa safu inayopangwa na mkuu wa nchi kuelekea michakato ya kisiasa inayohusika, Katiba Mpya, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Uchaguzi Mkuu na mabadiliko mbalimbali ya sheria za uchaguzi, wataalamu hao pia wametaka wateule wasigeuke machawa, badala yake wamshauri Rais ukweli.
Katika mazungumzo yake na Mwananchi jana, pamoja na kusifu uzoefu wa walioteuliwa, Mhadhiri Msaidizi wa Sayansi ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Revocatus Kabobe alishuku utendaji kama utakidhi matarajio ya Rais Samia.
Mashaka yake yanatokana na kile alichofafanua kuwa, baadhi ya wateule ni makada kindakindaki wa CCM, pengine wakakosa mawazo mbadala.
“Changamoto anayoiona ni kwamba wateule hawa ni wanaza wa CCM, sidhani kama watakuwa na mawazo mbadala na wakati mwingine watashindwa kumueleza ukweli wakihofia kupoteza nafasi zao,” alieleza.
Kwa mujibu wa Kabobe, walihitajika watu wasiofungamana na upande wowote wa kisiasa, kwa kuwa wana mitazamo ya kutoa maoni hasa mbadala.
“Kwa kuwa amekuwa akisimamia maridhiano angepata watu ambao hawana upande wowote ingekuwa bora zaidi, waliopo wanaweza kutomwambia ukweli wakihofu kupoteza nafasi zao.
“Akipatikana mtu ambaye haonekani kufungamana na chama chochote cha siasa, na mtazamo wa Rais wataendana,” alisema.
Kuhusu idadi ya walioteuliwa, Kabobe alisema ni utashi wa Rais kuamua idadi inayofaa kumsaidia, hivyo si tatizo wakiwa wengi.
Akitafsiri uteuzi huo, mhadhiri huyo alieleza ni maandalizi kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Uchaguzi Mkuu na michakato mingine ya kisiasa.
“Kwenye uchaguzi mkuu, kiongozi makini lazima apange safu ya kumpeleka kwenye tija ya siasa, tumeona amewaongezea hadhi ya ubalozi baadhi ya wasaidizi wake, ipo namna ama anawahamisha kupisha wapya au anawapa nguvu zaidi,” alisema.
Kwa sababu Serikali inaelekea kwenye mchakato wa Katiba Mpya, jambo linalohitaji muafaka wa kitaifa, Kabobe alisema mkuu wa nchi anahitaji watu wenye uwezo wa kumshauri namna ya kuyafikia hayo.
Tofauti na alichokisema Kabobe, Mhadhiri wa Rasilimali Watu na Utawala Bora kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDACo), Dk Lazzaro Swai alisema ubobezi wa walioteuliwa unatosha kuifanya kazi hiyo.
“Ilimradi walioteuliwa wana ubobezi kwenye maeneo husika, wanatosha kuifanya kazi hiyo.
“Siasa ni suala mtambuka, ukija kwenye uchumi kuna siasa, uhusiano wa kimataifa kuna siasa, siasa za ndani pia zinahusiana na siasa,” alisema.
Kuhusu idadi ya walioteuliwa, Dk Swai alieleza mtu mmoja hatoshi katika maeneo yote na walioteuliwa ni kutokana na uzoefu wao katika nafasi husika.
Lakini, aliweka wazi kuwa uteuzi huo unalenga ajenda zijazo za kisiasa alizonazo mkuu wa nchi, hivyo anahitaji wateule wamsaidie.
“Maridhiano kunahitajika mtu mwenye uwezo katika eneo hilo, pia wawe na uzoefu wa kutatua migogoro kwa kuwa tunaenda kwenye kipindi cha joto la siasa hasa kuelekea mchakato wa Katiba Mpya,” alisema.
Uteuzi wa wakongwe hao wa siasa ni turufu katika kutengeneza uelekeo wa kisiasa wa Rais Samia kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, kama inavyoelezwa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk Faraja Kristomus.
Hoja yake hiyo inatokana na alichokifafanua kuwa, Bulembo amewahi kuwa Meneja wa Kampeni wa Hayati John Mgufuli, kadhalika Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM.
“Uzoefu huo utamsaidia kumuunganisha Rais Samia na wazee na hata kumsaidia ushauri wa siasa za uchaguzi kwa sababu amewahi kuziishi alipokuwa meneja wa kampeni,” alisema.
Kwa upande wa Lukuvi, alisema ni mwanasiasa aliyekuwepo bungeni tangu mwaka 1995 na amekuwa ndani ya Serikali za awamu nne.
Uzoefu huo wa Lukuvi kwa mujibu wa Dk Kristomus, utamwezesha kumshauri mkuu wa nchi kwa kuwa anazijua siasa za ndani ya bunge, mifumo ya Serikali.
“Anaweza kumpa picha halisi ya nini kinahitajika anapotengeneza muelekeo wake wa kisiasa na Rajab amekuwepo katika siasa za ndani ya CCM, hivyo atamsaidia Rais Samia katika upande wa siasa ndani ya chama hicho hasa visiwani Zanzibar,” alisema.
Licha ya wateule hao kuwa turufu kwa Rais Samia, mhadhiri huyo alieleza kwa upande mwingine alihitajika kijana kuwa sehemu ya teuzi hizo ili kujenga uelewano na kizazi cha sasa.
“Kwa walioteuliwa kuna changamoto ya kupishana mawazo kati ya wateule na kizazi cha sasa cha wapiga kura ambao ni watu wenye rika kati ya miaka 20 hadi 40,” alisema.
Wasiwe ‘machawa’
Tofauti na maoni mengine, Mtaalamu wa Siasa na Uchumi, Profesa Joseph Mbwiliza aliwataka wateule hao waepuke kuwa ‘machawa’ wa mkuu wa nchi, akisisitiza kufanya hivyo si kumsaidia.
“Wasiwe machawa, maana mshauri wa rais ana nafasi kubwa katika jamii anaweza kumpotosha akasababisha mambo mengine, kwa kuwa Rais mwenyewe alishasema yupo tayari kukosolewa kwa staha wawe wakweli mbele yake,” alisema.
Kwa mujibu wa Profesa Mbwiliza, wateule hao wamepata nafasi nzuri ya kuongea na mkuu wa nchi faragha, wautumie uzoefu wao kumshauri Rais ukweli.
Katika kuyatekeleza majukumu hayo, aliwataka pamoja na vyanzo vingine wavitumie vema vyombo vya habari kama vyanzo vya taarifa kuhakikisha wanamshauri Rais yaliyopo nchini.
Aliwataka kuwa washauri wanaosikiliza kinachosemwa na wakosoaji na wasiwatafsiri kuwa wanapinga kwa kusaka madaraka.
“Kuna wazee unakuta wanashauri jambo, ukiweka mtazamo kwamba wanasema hivyo kwa hasira ya kutaka vyeo unakosea, unapaswa umsikilize kwa sababu wengine wanasukumwa na uzalendo wao. Kazi ya kumshauri Rais si uchawa,” alisema.
Huyu ndiye Lukuvi
Si jina geni masikioni mwa watu, amekuwa katika majukwaa ya kisiasa tangu mwaka 1995 aliposhinda ubunge wa Isimani mkoani Iringa, wakati huo pia aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Vijana na Kazi hadi mwaka 2000.
Amewahi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge na Uratibu kwa awamu mbili, kadhalika Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mwanasiasa huyo kwa vipindi tofauti amewahi kuhudumu wadhifa wa Mkuu wa Mkoa katika Mikoa ya Dodoma na Dar es Salaam, huku nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Bukoba.
Kinachotajwa ni mkongwe wa siasa si ndani ya Serikali pekee, Lukuvi amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM, ikiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Bulembo
Novemba mwaka 2012, ndipo jina la Bulembo lilianza kutambulika, baada ya kuukwaa wadhifa wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM.
Kujulikana kwake kuliongezeka zaidi pale, alipoteuliwa na Hayati Magufuli kuwa meneja wake wa kampeni za uchaguzi wa kuwania urais mwaka 2015.
Baada ya uchaguzi huo, Bulembo aliteuliwa na Hayati Magufuli kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wadhifa aliodumu nao kwa miaka mitano.
Luhwavi
Mwaka 2017 hadi 2020, Luhwavi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, kabla ya hapo alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Bara.
Kadhalika, Balozi Luhwavi amewahi kuwa msaidizi wa Hayati Magufuli katika eneo la siasa kwa miaka mitano, wadhifa ambao alikuwa nao hata kabla.
Haji Omar Kheir
Ni kiongozi mwandamizi aliyehudumu nyadhifa mbalimbali ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ikiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum.
Amewahi pia kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Huduma za Jamii na Utawala Bora visiwani Zanzibar, wakati huo akiwa mjumbe wa baraza la wawakilishi. |
Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Sweden, Dk Willibrod Slaa amesema upinzani wake dhidi ya mkataba | Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Sweden, Dk Willibrod Slaa amesema upinzani wake dhidi ya mkataba wa ushirikiano wa uendeshaji Bandari kati ya Kampuni ya DP World na Tanzania, haulengi kukataa wawekezaji, huku akiishauri Serikali irekebishe kasoro zinazolalamikiwa.
Hoja hiyo ya Dk Slaa inapigia msumari ile iliyoibuliwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) juzi, likiitaka Serikali kwenda kwa wananchi kuwafafanulia vifungu vyote vilivyoibua mijadala ili kuwatoa hofu na kurekebisha kasoro zitakazobainika.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Dk Slaa jana alisema hapingi kulenga kuwakataa wawekezaji, bali analenga maslahi ya taifa.
“Naomba ieleweke bila chembe ya wasiwasi wowote kuwa, taarifa hii haina dhamira yoyote ya kupinga uwekezaji wa kweli na wenye tija kwa manufaa ya taifa letu,” alisema.
Hata hivyo, alieleza mashaka yanayoibuka kutoka kwa wananchi, yanatokana na rejea ya mikataba mbalimbali ambayo Serikali iliwahi kuingia na mataifa mengine na ikaleta changamoto.
Aliitaja mikataba hiyo ni Serikali na Symbion Power Tanzania Limited, Richmond, IPTL na mingine.
Usiri uliogubika mchakato wa mkataba huo, ni miongoni mwa kasoro zilizotajwa na Dk Slaa, akisisitiza hakukuwa na sababu ya wananchi kupata taarifa baada ya kuvuja.
“Kwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan alionekana akishuhudia uwekaji saini wa mkataba, ni busara ya kawaida taifa kuarifiwa juu ya mikataba hiyo,” alisema.
Kwa upande wake, Mtaalamu wa Sheria za Kimataifa, Wakili Peter Madereka alisema Serikali inapaswa kutoa elimu kwa wananchi, badala ya kumuita mkosoaji mmoja mmoja.
“Endapo kila mmoja atapata ukweli wa jambo hakuna atakayeitwa mpotoshaji, mashaka yaliyopo yametokana na masuala ya kisheria,” alisema.
Katika mkataba huo, ambao tayari umesharidhiwa na bunge, Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe alitaka umiliki wa 50 kwa 50 kati ya DP World na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).
Hata hivyo, Kabwe alisema kilichopitishwa na bunge ni azimio la ushirikiano baina ya nchi mbili ambalo lisipotekelezwa kwa miezi 12 linakufa.
Kwa mujibu wa Kabwe, kwa kuwa asilimia 67 ya mauzo ya nje ya Dubai ni jiografia yao, ni muhimu kushirikiana nao sawa, ili kujenga uwezo wa ndani na baada ya kuwa na uwezo itakuwa rahisi kuwanunua kwa asilimia 100.
“Nimetazama takwimu na tija ya bandari yetu -tunaweza kufuta kodi zote nchini tukabakiza ushuru wa forodha tu bandarini na nchi ikaenda,” alisema.
Kuhusu Zanzibar: “Bandari ni jambo la muungano Lakini kama ilivyo mafuta na gesi utekelezaji wake sio wa muungano. Zanzibar wana shirika lao la Bandari. Kwa Mujibu wa Sheria yetu ya bandari hata Mtwara inaweza kuwa na kampuni yake ya kujiendesha,” alisema.
Kwa ujumla wake, alisema kinachohitajika ni kampuni ya uendeshaji wa bandari imilikiwe asilimia 50 kwa 50 kati ya TPA na DP World na inaweza kuitwa Tanzania-Dubai Ports Limited (TDPL).
Jambo lingine, alisema ni mkataba wa uendeshaji wa bandari uingiwe kati ya TPA na hiyo Kampuni ya ubia na lingine ni DP World isifanye uwekezaji wowote kwenye bandari za nchi jirani bila kwanza kujadiliana na Serikali ya Tanzania.
Kauli ya LHRC
Katika hatua nyingine, katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga aliitaka Serikali irejee upya vipengele vya mkataba vyenye changamoto ya kisheria hasa vilivyoibua mijadala.
Si masuala ya kisheria pekee, Anna alitaka hata kiwango cha umiliki wa sehemu ya uwekezaji kiwekwe wazi, ili wananchi waelewe faida itakayopatikana.
"Ni vema kuendelea kwa uwazi wa mikataba ya kiuwekezaji inayohusu maslahi mapana kwa taifa kama ilivyojitokeza katika mkataba huu kati ya Serikali na DP World," alisema Henga.
Ushirikishwaji wa wananchi ni jambo lingine alilolitaja Anna kuwa lilipaswa kufanyika, akieleza katika mkataba huo uliopitishwa na Bunge Juni 10, mwaka huu hakukuwa na ushirikishwaji.
Mwisho.
Kutokana na kuimarika kwa matumizi ya teknolojia katika sekta ya Usafiri wa Anga, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete amesema mapato yameongezeka maradufu kwa Serikali.
Uimara huo wa teknolojia unaoelezwa na Mwakibete unahusisha matumizi ya vifaa vya kidigitali vinavyowezesha kuonekana kwa ndege yoyote inayofanya safari katika anga la Tanzania.
Akizungumza katika mkutano wa wadau wa huduma za uongozaji ndege uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, Mwakibete alisema kwa mwaka huu wa fedha Sh83 bilioni zinatarajiwa kukusanywa.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, fedha hizo zinatarajiwa kukusanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) ikiwa ni matokeo ya kuimarika kwa teknolojia.
"Tumeimarisha matumizi ya teknolojia na kuwezesha kuongeza makusanyo ya mapato ndani ya TCAA," alisema.
Alieleza kwa sasa tayari zaidi ya Sh70 bilioni zimeshakusanywa na kwamba TCAA imejiwekea lengo ya kukusanya Sh87 bilioni katika mwaka wa fedha ujao.
Kiasi hicho cha fedha kinachokusanywa sasa, Mwakibete alisema hakilingani na kilichokusanywa kabla ya uwepo wa teknolojia hizo.
"Kabla ya matumizi ya teknolojia, TCAA ilikuwa ikikusanya Sh24 bilioni kwa mwaka mmoja wa fedha," alisema.
Akifafanua maboresho ya teknolojia hizo, Kaimu Mkurugenzi wa TCAA, Daniel Malanga alisema rada nne zilizonunuliwa zimechagiza hayo.
Alieleza kabla ya kuwepo kwake, mashirika mbalimbali ya Ndege yalikuwa na uwezo wa kufanya safari kupitia anga la Tanzania bila kujulikana.
"Hilo linaikosesha Serikali mapato, lakini kwa sasa hakuna Ndege itapita katika anga letu bila ya sisi kujua," alisema.
Akizungumzia mkutano huo, Malanga alisema mwaka huu wadau kutoka ndani na nje ya nchi wamealikwa kushiriki.
Mkutano huo wa siku mbili, alieleza utahusisha mazungumzo mbalimbali ya kubadilishana uzoefu ili kuimarisha usalama wa anga la Tanzania.
"Usalama wa anga unaongeza mapato ya Serikali kwa kuwa ndege nyingi zitavutiwa kutumia anga la Tanzania," alisema.
Hata hivyo, alisema ni mkutano wa kubadilishana uzoefu wa mifumo ya nje ili kujifunza teknolojia mpya za kuongoza Ndege.
Mkurugenzi wa Huduma za Uongozaji Ndege TCAA, Floral Alphonce alisema kwa sababu dunia inakwenda katika digitali ni vema sekta hiyo ikajielekeza huko.
Mkutano huo utafanyika siku mbili, huku kauli mbiu ikiwa ni 'Kuimarisha mifumo ya uongozaji ndege kwa ajili ya uendelevu wa sekta ya anga Tanzania.' |
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema ameutaka uongozi wa Seneti y | Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema ameutaka uongozi wa Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu ya chama hicho, kuandaa kanzidata ya wahitimu wa elimu ya juu.
Kwa mujibu wa Mjema, kanzidata hiyo itarahisisha kuwapata wataalamu wa kada mbalimbali zinapotokea fursa.
Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana, alipohutubia mahafali ya seneti ya vyuo na vyuo vikuu ya Mkoa wa Dar es Salaam.
“Katika risala yenu nimesikia mmeomba kupewa kipaumbele katika fursa za ajira, kwa jambo hilo naomba muandae kanzidata ili iwe rahisi kuwapata,” alise,a.
Alisema kanzidata hiyo itasaidia hata katika kuwaunganisha wahitimu hao katika mafunzo taratali kupitia Wakala wa Ajira Tanzania (TaESA).
Hata hivyo, alisema itakapoandaliwa kanzidata hiyo, atahitaji kukutana na wahitimu hao kabla ya mwishoni mwa Julai kwa mazungumzo kuhusu mambo mbalimbali.
Katika hatua nyingine, Mjema alisema kusoma kwao hakujalenga maslahi yao pekee, bali familia zao na jamii inayowazunguka.
"Elimu uliyoipata kaitumie kwa matumizi chanya, tunataka ninyi muwe nyenzo ya mabadiliko," alisema.
Kadhalika, alitaka kusoma kusiwe sababu ya kuwa wapinzani wa kila jambo, kwa kuwa kufanya hivyo hakuna hatma nzuri.
"Ukiangalia wengi wenu hapa mliohitimu mna zaidi ya miaka 20 ya kuendelea kukua, unaweza kuwa mpinzani lakini angalia maisha yako yanaishiaje," alisema.
Aliisisitiza hoja yake hiyo kwa kufananisha na taifa la China, akisema kila eneo utakalotembelea katika nchi hiyo wananchi wake wanazungumza maendeleo.
"China kila unapokwenda wanazungumza jambo moja la kujenga nchi, kuleta maendeleo ili wawe wa kwanza," alieleza.
Aliwahakikishia baadhi ya wahitimu hao, kupata fursa katika mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) kwa awamku zijazo, akijibu ombi katika risala iliyosomwa na wanafunzi hao.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Nasra Ramadhan alisema wakati wote vijana watamuunga mkono mkuu wa nchi, Rais Samia Suluhu Hassan.
Alisema uamuzi wa kumuunga mkono unatokana na juhudi anazofanya katika kuiletea nchi maendeleo. |
Unatumia kipimo gani kuthibitisha ubora wa tofali za mchanga kwa ajili ya ujenzi wa nyumba yako? una | Unatumia kipimo gani kuthibitisha ubora wa tofali za mchanga kwa ajili ya ujenzi wa nyumba yako? unafahamu athari za kutumia tofali hizo kiholela katika ujenzi?
Maswali haya ni machache kati ya mengi yanayopaswa kuulizwa hasa katika kipindi hiki ambacho maeneo mengi nchini ikiwemo Dar es Salaam, kumeibuka idadi kubwa ya viwanda vya tofali za mchanga.
Ingawa wingi wa viwanda hivyo, unarahisisha upatikanaji wa bidhaa hiyo, kadhalika kupunguza bei yake kutokana na ongezeko la ushindani, ubora wa tofali zinazozalishwa unabaki kuwa kitendawili kisichoteguka.
Kwa taarifa yako! kuigonga tofali, kuangalia mvuto wake, nakshi za migongo na kunyooka kwake si ithibati ya ubora wa bidhaa hiyo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba yako, kulingana na wataalamu.
Gazeti la Mwananchi limetembelea viwanda mbalimbali vya tofali jijini hapa na kubaini idadi kubwa havifuati mbinu za kitaalamu katika uzalishaji wa bidhaa hiyo, jambo linaloelezwa na wataalamu kuwa linahatarisha makazi hasa wakati wa majanga likiwemo tetemeko la ardhi.
Kwa mujibu wa Mtaalamu wa ujenzi, Mhandisi Barakael Mmari, tofali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba inapaswa kuwa na ubora utakaohimili mgandamizo wa kuanzia Mega Pascal 4 (4MPA).
Hiyo ni sawa na kile alichofafanua kuwa, ubora huo utapatikana iwapo mfuko mmoja wa saruji utatumika kuzalisha tofali kati ya 25 hadi 30 za mchanga.
"Kama ni kwa ajili ya nyumba zetu za kawaida, tofali hazibebi mzigo mkubwa, hivyo zinazohimili mkandandamizo wa kuanzia 4MPA na kuendelea zinafaa.
"Yaani zilizotengenezwa kwa mchanga na mfuko mmoja wa saruji kutoa tofali kati ya 25 na 30," anafafanua Mhandisi Mmari ambaye pia ni Meneja wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka kutoka Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads).
Hata hivyo, Mhandisi huyo anasema ubora wa tofali unabadilika kulingana na matumizi yanayokusudiwa, akifafanua shughuli nyingine huhitaji ziongezwe ubora kwa kuchanganywa na kokoto.
Ufafanuzi wa Mmari, unawekewa msisitizo na Mhandisi Vicent Tarmo anayesema tofali hizo zimegawanyika katika makundi mawili yaani inchi tano na sita.
Tofali za inchi sita, Mhandisi Tarmo anasema hutumika kujenga misingi ya majengo, wakati inchi tano zikitumika kukamilisha ujenzi wenywewe.
“Ubora wa tofali hutegemea na mchanganyiko wa malighafi zinazotumika kwa maana ya mchanga, saruji na maji,” anasema Mhandisi Tarmo.
Anataja ubora unaokubalika kwa tofali za inchi tano ni mchanganyiko wa mfuko mmoja wa saruji, ndoo ndogo angalau 43 za mchanga na tatu za maji.
“Katika mchanganyiko huo utapata tofali takriban 38 imara na bora,” anasema.
Anaeleza kipimo cha ubora wa tofali hizo ni Newton 3.6 kwa milimita ‘square’.
Hilo linaungwa mkono na Mhandisi Joseph Rwihura anayesema kwa msingi wa nyumba tofali zinazostahili ni zile zilizofyatuliwa 25 hadi 30 kwa mfuko mmoja wa saruji.
Tofauti na msingi wa nyumba, anaeleza kwa mfuko mmoja wa saruji zikifyatuliwa 30 hadi 40 zinafaa kuendeleza ujenzi wenyewe.
Kulingana na Mhandisi huyo aliyehudumu Tanroads kwa miongo kadhaa tangu ilipoanzishwa, ni hatari iwapo msingi wa nyumba utajengwa kwa tofali zenye ubora chini ya alivyoeleza.
Kinachoelezwa na Rwihura, kinaungwa mkono na Mhandisi Leonard Saukwa anayesema mfuko mmoja wa saruji unatakiwa kuzalisha tofali zisizozidi 35 tu.
Uhalisia viwandani
Wakati wataalamu wakieleza hayo, uhalisia wa viwango vya ubora wa tofali zinazozalishwa viwandani ni tofauti.
Katika viwanda 10 vilivyotembelewa na mwandishi wa habari hii, katika Jiji la Dar es Salaam ni viwili ndivyo vinavyozalisha bidhaa hiyo kulingana na ilivyoelezwa na wataalamu.
Kimoja kinazalisha tofali 35 na kingine kwa mfuko mmoja wa saruji, huku vilivyobaki vikizalisha kuanzia tofali 50 na zaidi kwa mfuko mmoja wa saruji.
Akizungumza na gazeti hili, mmiliki wa kiwanda hicho kinachozalisha tofali 35 kwa mfuko mmoja Damian Liundi, anasema tofali moja yenye ukubwa wa inchi sita huuzwa Sh1,250 huku inchi tano ikiuzwa Sh1,150.
"Bei hizi unaleta mzigo popote ulipo ndani ya Dar es Salaam, ukifuata bei inapungua kutoka Sh1,250 kwa inchi sita hadi Sh1,100 hukuinchi tano ikipungua kutoka Sh1,150 hadi Sh1,050," anasema.
Lakini, anabainisha bei hutofautiana kulingana na umbali wa yanakopatikana malighafi hasa mchanga.
Kingine kinazalisha tofali 30 kwa mfuko mmoja wa saruji na kulingana na mafundi waliokuwa kiwandani hapo, hakuna mafunzo katika shughuli hiyo ni uzoefu.
Selemani Said mmoja wa mafundi hao anasema kiwango cha tofali wanachozalisha kwa mfuko mmoja wa saruji ni maelekezo ya mwajiri wao.
"Maelekezo ya bosi ni kwamba kiwanda chake, anataka mfuko mmoja wa saruji uzalishe tofali 30 na ndivyo tunavyofanya," anasema.
Alipoulizwa iwapo amewahi kuhudhuria mafunzo yoyote ya shughuli hiyo, Said anaeleza amewahi kusikia, aghalabu ikitokea bosi wake ndiye anayekwenda.
Katika moja ya kiwanda, Mwembechai jijini hapa, mfuko mmoja wa saruji huzalisha tofali 50.
Mmoja wa mafundi katika kiwanda hicho, anasema anachofahamu ni mfuko mmoja 2a saruji unapaswa kutoa tofali 50.
"Hii kazi hauendei shule unajua, unafika kiwandani unawakuta wakongwe wanakupa maelekezo unajifunza ukizoea unafanya mwenyewe.
"Suala la idadi ya tofali kwa mfuko ni mipango ya bosi, lakini unaona mwenyewe tuna tofali ngumu," anaeleza.
Katika viwanda vyote vilivyotembelewa na gazeti hili, imebainika kuwa uamuzi wa idadi ya tofali kwa mfuko mmoja wa saruji ni maamuzi ya mmiliki.
Juma Mussa wa kiwanda kingine cha tofali kutokea Temeke jijini hapa, anasema bosi ndiye mwenye mamlaka ya kuamua idadi ya tofali kwa mfuko wa saruji, lakini chini ya ushauri wa fundi mkuu.
"Kwa sababu bosi anataka hela anaweza kusema hata mfuko mmoja kwa tofali 100, hapo ndipo fundi mkuu anaposhauri kwamba asizidishe tofali zitakuwa mbaya," anasema.
Kugongagonga, kuinyanyua na mwonekano, bado vinaendelea kutumika kama vipimo vya ubora wa tofali, kulingana na baadhi ya wananchi.
“Utajuaje kama hii tofali bora kama haujaigonga au kuinyanyua uone uzito wake? Kuna nyingine ukinyanyua inakatika, zipo nyingine zinamung’unyuka,” anasema Marco Manembo mkazi wa Dar es Salaam.
Anaeleza ugumu wa kujua ubora wa tofali kwa viwango vinavyoelezwa, akisisitiza wakati zinafyatuliwa mteja huwa hayupo.
Hatari inayotarajiwa
Iwapo zitatumika tofali zisizo na ubora, Mhandisi Tarmo anasema kuna hatari ya jengo kutengeneza nyufa kwa kushindwa kuhimili mgandamizo.
“Nyumba iliyojengwa kwa kuzingatia viwango bora vya matofali huweza kudumu kwa zaidi ya miaka 50 bila matengenezo,” anasema.
Anapendekeza kabla ya kuanza ujenzi ni vema kuthibitisha ubora wa tofali unazotumia kwa kuchukua sampuli na kupeleka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa ajili ya uhakiki.
“TBS ndiyo wenye vipimo vya ubora,” anaeleza Mhandisi Tarmo.
Kwa upande wake, Mhandisi Mmari anasema ubora wa nyumba unatokana na msingi imara, miranda na ring beam ‘rinta’ (zege inayozungushwa kabla ya nyumba kukamilika).
“Mara nyingi nyufa hutokana na msingi kutokuwa imara, ubora wa tofali za msingi huo ni jambo muhimu kwenye kudhibiti hili. Vilevile nyumba isipokuwa na miranda, ring beam, inaweza kusababisha mipasuko,” anafafanua.
Anaeleza hatari inakuwa kubwa zaidi iwapo nyumba imejengwa kwa tofali zisizo na ubora na likatokea janga kama tetemeko.
Kauli ya Serikali
Akizungumzia hilo, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dk Ashatu Kijaji anasema kinachofanywa na Serikali ni kutoa elimu kwa wazalishaji wa bidhaa hiyo kuhakikisha wanazingatia ubora.
Elimu hiyo, kwa mujibu wa Dk Ashatu inatolewa na TBS, kadhalika linafanya ukaguzi wa kawaida na kustukiza katika jitihada za kuhakikisha viwango vinafuatwa.
“Shirika linaendelea kutoa elimu kwa wazalishaji wa tofali sambamba na kufanya ukaguzi wa kawaida na wa kustukiza katika jitihada za kuhakikisha wazalishaji wanakidhi viwango vya uzalishaji bora wa bidhaa za matofali ya mchanga,” anasema.
Kwa mwaka huu wa fedha, Dk Ashatu anasema semina moja imefanywa kila kanda na kaguzi tano nchi nzima, huku mwaka wa fedha ujao TBS ikitarajia kuongeza mikakati ya kutoa elimu kupitia Luninga. |
Hatma ya uamuzi wa ama kuadhibiwa au vinginevyo kwa Balozi Ali Abeid Karume kwa tuhuma za kuitukana | Hatma ya uamuzi wa ama kuadhibiwa au vinginevyo kwa Balozi Ali Abeid Karume kwa tuhuma za kuitukana CCM na viongozi wake, ipo mikononi mwa uongozi wa chama hicho katika tawi la Mwera anakoishi.
Hilo linatokana na taarifa kuwa, juzi mwanasiasa huyo aliitwa na uongozi huo kwa mahojiano marefu na kinachosubiriwa ni ripoti ya mazungumzo hayo kwa ajili ya hatua.
Wito wake mbele ya uongozi wa tawi hilo, umechagizwa na kile kilichoelezwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi juzi aliyetaka hatua dhidi ya wanachama wanaokiuka maadili ya chama hicho.
Katika ziara yake ya kukagua miradi, Dk Mwinyi alisema: “Wakati mwingine watu wanavunja maadili lakini wanatazamwa na kusubiriwa kwenye uchaguzi.
“Huo sio utaratibu tuanze sasa, wanaofanya hivyo washughulikiwe kwa mujibu wa taratibu na ndiyo maana kuna kamati za maadili ndiyo kazi yao,” alisema Dk Mwinyi ambaye pia ni Rais wa visiwa hivyo.
Kinywa ndicho kilichomponza Balozi Karume hadi inafikiwa hatua hiyo, ingawa mwenyewe anakana kutoa lugha ya matusi dhidi ya CCM na viongozi wake.
Mara kadhaa, mwana huyo wa Rais wa kwanza wa visiwa hivyo, Hayati Abeid Amani Karume amekuwa akiituhumu CCM kuingia madarakani kwa wizi wa kura.
Hata hivyo, Rais Mwinyi alipoeleza kuhusu uwepo wa wanasiasa wanaoitukana CCM na viongozi wake, Balozi Karume alikana katu kulifanya hilo.
Akijibu maswali yaliyotumwa kwake na gazeti hili jana, Balozi Karume alisema mazungumzo marefu na uongozi wa tawi CCM katika tawi lake, wamekubaliana kwamba hakutukana.
Mwanasiasa huyo alikiri kuwa mwanachama yeyote atakayekiuka maadili kwa kutukana chama na viongozi wake lazima ashughulikiwe.
Lakini, alisema: “Jana (juzi) niliitwa na uongozi wa tawi langu. Baada ya mazungumzo marefu tumekubaliana kwamba sijatukana chama wala viongozi. Mhusika asubiri ripoti ya hao aliowatuma kushughulikia suala hilo.”
Alipoulizwa iwapo atakuwa tayari kuomba radhi, alijibu atafanya hivyo baada ya kuambiwa kosa lake na kama litakidhi kuwa tusi kwa CCM na viongozi wake.
“Nikiambiwa kosa langu na kukidhi kuwa hilo nililosema ni tusi au matusi kwa chama na viongozi wake, kuomba radhi ni uungwana,” alisema.
Kwa mujibu wa Balozi Karume, amewasiliana na Katibu wa Kamati Maalum ya Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar, Khamis Mbeto na kukubaliana utayari wake wa kwenda kutoa maoni yake.
“Nimemsikiliza Mbeto na nimewasiliana naye. Tumekubaliana kwamba naweza kwenda kwao saa yoyote kutoa maoni yangu. Amenihakikishia kwamba matusi ya kiongozi wa CCM kwamba mimi ni mlevi na mwendawazimu, sio kauli ya chama,” alisema.
Alipoulizwa kuhusu kuwahi kuwasiliana na viongozi wa CCM wajirekebishe kuhusu anayoyasema, alijibu hana uhalali wa kushiriki vikao nao kwa kuwa si mjumbe na hata alipoomba nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) iliagizwa jina lake likatwe.
Pamoja na kauli kali za Dk Mwinyi dhidi ya wanaokiuka maadili, Balozi Karume alisema haoni sababu ya kufikiwa kwa uamuzi way eye kufukuzwa ndani ya chama hicho.
“Tusubiri kama nitafukuzwa. Lakini mimi sijaiona sababu ya kufikia hatua hiyo,” alisema.
Kauli ya CCM
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Mbetto alisema kwa kuwa Balozi Karume kwa sasa hana uongozi wowote ndani ya CCM na Serikali, mchakato wa kuhojiwa kwake unaanzia ngazi ya tawini kwake.
Alieleza tawi litatoa mapendekezo yake kwa wadi juu ya adhabu anayopaswa kuchukuliwa na ngazi ya mwisho ya kumchukulia hatua ni Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa anaoishi.
“Halmashauri Kuu ya Mkoa ina nguvu ya kumchukulia hatua hata ya kumfukuza uanachama,” alisema.
Alieleza angekuwa ni kiongozi kati ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC), Mwakilishi au CCM Wilaya, maamuzi yoyote dhidi yake yangefanyika na mamlaka za chama hicho kitaifa. |
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameondoka nchini kuelekea nchini Italia kwa ziara ya kikazi ya | Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameondoka nchini kuelekea nchini Italia kwa ziara ya kikazi ya siku nne.
Katika safari hiyo, Mbowe ameambatana na viongozi wengine wawili wa chama hicho, Makamu Mwenyekiti Bara, Tundu Lissu na Katibu Mkuu, John Mnyika.
Hayo yameelezwa leo, Juni 5, 2023 katika taarifa kwa umma iliyotolewa na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema.
Kwa mujibu wa Mrema kupitia taarifa hiyo, Lissu na Mnyika watatangulia kurejea nchini Juni 7, mwaka huu wakati Mbowe akiendelea na ziara kwingineko.
Imeelezwa kwa Mwenyekiti huyo baada ya kuhitimisha ziara ya Italia, atakwenda Ujerumani kwa ziara ya siku mbili.
Atakapokuwa Ujerumani kulingana na taarifa hiyo, atakutana na viongozi mbalimbali wa kisiasa, Serikali na Mashirika ya Kimataifa na kwamba atarejea nchini Juni 10 mwaka huu. |
Hatua ya Serikali kuchelewa kuwapangia shule wanazopaswa kwenda wanafunzi wanaotarajia kujiunga na k | Hatua ya Serikali kuchelewa kuwapangia shule wanazopaswa kwenda wanafunzi wanaotarajia kujiunga na kidato cha tano, imeibua wasiwasi kwa wazazi, wakieleza hilo linawapunguzia muda wa kujiandaa.
Wasiwasi huo wa wazazi, unatokana na ukweli kwamba licha ya matokeo ya mtihani wa kidato cha nne kutangazwa Januari 29, mwaka huu, hadi sasa wanafunzi hao hawajapangiwa shule wanazopaswa kwenda kujiunga.
Kinacholalamikiwa zaidi ni utaratibu wa siku zote ambao aghalabu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) huwapangia wanafunzi shule mwezi Mei, tofauti na mwaka huu.
Kuchelewa huko kumesababisha baadhi ya watoto kuwa na hofu juu ya hatma ya elimu zao, kama inavyoelezwa na Mussa Mbwana mzazi wa mmoja wa wanafunzi.
“Mwanangu amesubiri hadi amekata tamaa, siku zote anakuwa na shauku ya kujua shule gani amechaguliwa kwenda lakini amesubiri hadi sasa na hana tena molari ya shule, simsikii akizungumzia shule,” alisema.
Hata hivyo, Katibu Mkuu Tamisemi, Adolfu Nduguru alisema bado kuna muda wa kutosha wa kulitekeleza hilo, akisisitiza likishatekelezwa wataweka pia kwenye tovuti za wizara.
“Ni hivi hatujatangaza na tukitangaza tutaweka kwenye website (tovuti) pia. Lakini kuhusu kuchelewa sijaelewa inamaanisha nini maana bado tuna muda wa kutosha wa kutangaza najua inawezekana,” alisema.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mzazi mwingine, Mwantumu Milanzi wa Dar es Salaam, alisema kutokana na hali yake ya maisha angetamani kujua mapema kwamba wapi mwanawe amepangiwa kwenda kusoma kidato cha tano.
“Wanasema elimu bila malipo sawa, wanawanunulia watoto na sare za shule? Maana kila shule ina rangu yake ya sketi au suruali, huwezi kununua mapema kwa sababu hujui mtoto amepangiwa shule gani na huwa wanavaa rangi gani,” alieleza.
Kwa kipato chake, Mwantumu alisema alipaswa kupokea taarifa mapema zaidi, lakini kinachofanyika sasa kinamfanya ashindwe kuvumilia kuhifadhi fedha hadi siku mwanawe atakapopangiwa.
Dala Malimi alieleza kwa kadri Serikali inavyochelewa kuwapangia wanafunzi shule wanazopaswa kwenda na ndivyo wanavyowaondoa wanafunzi katika hali ya usomi.
“Mtoto ameiandaa saikolojia yake kusoma, unapomchelewesha anatoka kwenye reli mwisho wa siku akirudi shuleni anakuwa kama haelewi, hata kama wataanza shule siku waliyopangiwa, lakini kuna haja ya kumuandaa kisaikolojia ajue shule gani atasoma,” alisema.
Harold Misungwi alisema kuchelewa huko kunasababisha sintofahamu kwa mzazi na mwanafunzi, kwa kuwa inachelewesha muda wa maandalizi.
“Wanavyochelewa ikitokea mtoto hajapangiwa shule, inakubidi mzazi umtafutie shule binafsi, kwa muda utakaobaki pengine mwezi mmoja unapata wapi hiyo hela ya kulipia shule binafsi,” alisema.
“Serikali inajua ratiba nzima ya mitihani na inatoa matokeo mapema, iwe na utaratibu wa kuwapangia wanafunzi shule wanazopaswa kwenda mapema ili wazazi tujiandae,” alisema.
Wadau wa elimu
Akizungumzia hilo, Mchambuzi na Mtafiti wa masuala ya Elimu, Muhanyi Nkoronko alisema licha ya elimu ya kidato cha tano na sita kuwa bila malipo, kunahitajika maandalizi.
Alieleza kuchelewa au ukimya wa mamlala kuhusu kupanga wanakopaswa kwenda wanafunzi, unawaweka wazazi njiapanda wasijue wapi watoto wao watapangiwa.
“Sawa elimu bila malipo, lakini shule hasa za bweni zinahitaji maandalizi mfano nauli, fedha ya mwanafunzi kujikimu, haya yote ni maandalizi yanayohitaji mzazi kuwa na taarifa mapema ili ayafanye,” alisema.
Si wazazi pekee, watoto nao, Nkoromo alieleza wanakuwa na mawazo mtambuka ya kutofanya uchaguzi sahihi.
Mdau huyo wa elimu, alifafanua wanafunzi wengi huamua kuendelea na kidato cha tano ama kujiunga na elimu ya ufundi au chuo cha kati, baada ya kujua shule walizopangiwa.
“Kuchelewa kupangiwa inawaacha kwenye mawazo wasijue mapema kwamba watakwenda kufanya nini, shuleni au wataenda chuo cha kati,” alisema.
Kinyume na mtazamo huo, Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu Kishiriki cha Eimu (DUCE), Dk Almas Mazige alisema hakuna tatizo kwenye jambo linaloendelea, kwa kuwa elimu ya ngazi hiyo kwa sasa hutolewa bila malipo.
“Hawa (Serikali) hawajaeleza lini wanatangaza, ukilaumu wakatangaza wiki ijayo na wakasema tunawapa mwezi na nusu wa kujiandaa hoja haitakuwa na maana,” alisema.
Ni mapema kutilia shaka kwa sababu, alisema haijulikani nini kinaifanya Serikali kuchelewa kutoa, lakini nini inatarajia kuja nacho.
“Kwa sasa kuna Katibu Mkuu mpya pengine amekuja na mabadiliko, maana yamewahi kufanyika mabadiliko mara kadhaa,” alifafanua Dk Mazige.
Mtaalamu wa Sera, Mipango na Utawala wa Elimu kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Winfrida Malingumu alisema kuchelewa huko kunasababisha wazazi wachague kuwapeleka watoto wao katika shule binafsi.
“Kwa sababu anakuwa na msongo wa mawazo na anakosa uhakika kama mwanawe atachaguliwa au laa, kwa hiyo njia pekee ya uhakika ni kumpeleka shule binafsi na huko anakwenda kuingia gharama,” alisema.
Wazazi kushindwa kujipanga ni suala linaloibuliwa pia na Dk Winfrida, akifafanua hata mtoto akikosa shule ya umma kama taarifa zimechelewa hatakuwa na uwezo wa kubadili uamuzi wa kumpeleka shule binafsi haraka kwa kuwa inahitaji kujipanga. |
Uchunguzi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), umebaini kifo cha mwanafunzi wa Chuo | Uchunguzi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), umebaini kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Nusura Abdallah hakihusiani na ajali iliyomhusisha Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Dk Festo Dugange.
Kifo cha mwanafunzi huyo kilitokea mapema Mei mwaka huu, huku mitandaoni zikisambaa taarifa zilizohusisha kifo hicho na ajali aliyopata Dk Dugange.
Kutokana na taarifa na utata wa kifo chake, Mei 10, mwaka huu THBUB ilitoa taarifa kupitia vyombo vya habari ikieleza nia ya kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kwa mujibu wa tume hiyo, tayari imeukamilisha.
Hayo yamebainishwa leo, Juni 2, 2023 katika taarifa ya matokeo ya uchunguzi iliyotolewa na THBUB kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Mwenywekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu, Mathew Mwaim.
Taarifa hiyo inabainisha ajali ya Dk Dugange ilitokea Aprili 25, 2023 usiku wa kuamkia Aprili 26 2023, maeneo ya Iyumbu, karibu na njia panda ya Shule ya Mfano, jijini Dodoma ambapo gari iliacha njia, kugonga mti na kupinduka.
“Baada ya kupata majeraha kutokana na ajali hiyo, Dk Dugange alihangaika kutafuta msaada wa kufikishwa hospitali kupata matibabu. Alfajiri Aprili 26, 2023 alisaidiwa na bodaboda iliyomfikisha Hospitali ya Benjamin Mkapa,” inaeleza taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, safari ya Nusura kwenda Moshi mkoani Kilimanjaro ilianza Aprili 27, 2023 kwa basi la Manning Nice baada ya gari la Kapricon alilopanga kusafiria awali kuchelewa.
Inaeleza basi hilo lilimfikisha Babati na baadaye alipanda Coaster hadi Arusha, kisha kumalizia safari yake hadi Moshi kwa basi la Ibra Line.
Baada ya kufika saa tano usiku, kwa mujibu wa taarifa hiyo, Nusura alipokelewa na mchumba wake, Juma Mohamed Kundya mjini Moshi hadi nyumbani.
“Lengo la safari hiyo lilikuwa ni kuzungumzia masuala ya uchumba wao na kupanga siku ya mchumba wake kwenda kujitambulisha nyumbani kwao Singida. Aidha, alipanga kukaa hapo hadi Mei 2, 2023 ndipo arejee Dodoma,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Kulingana na taarifa hiyo, Nusura aliwasiliana kwa mara ya mwisho na familia yake, Aprili 29, 2023 na Mei 1, 2023 ilikuwa mara ya mwisho kuwasiliana na rafiki anayesoma naye chuoni.
Siku hiyo, taarifa hiyo inaeleza aliandaa chakula cha jioni walichokula na mchumba wake na mpwa wa mchumba huyo.
Baada ya kumaliza kula, taarifa inaeleza Nusura alijisikia vibaya na kuanza kutapika hadi kuishiwa nguvu hali iliyosababisha kufikishwa Hospitali ya Faraja kwa matibabu.
“Pamoja na hatua mbalimbali za kitabibu zilizochukuliwa na Madaktari wa Hospitali hiyo, Nusura alifariki dunia saa 5:00 usiku wa Mei 1, 2023,” inaeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inabainisha vipimo vilivyofanywa na hospitali hiyo vinaonyesha kifo chake kimetokana na shambulio kali la kupanda kwa sukari na upungufu wa damu.
Hata hivyo, daktari aliyempatia huduma na ndugu wa marehemu walioutayarisha mwili kwa ajili ya mazishi walithibitisha kutokuwepo kwa majeraha.
Hakukuwa na sumu kwenye mabaki ya chakula na matapishi ya Nusura baada ya vipimo vilivyofanywa na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, inaeleza taarifa hiyo.
Kuhusu ajali, taarifa inabainisha ilihusisha gari binafsi aina ya Toyota Land Cruiser GXR V8 yenye namba za Usajili T454 DWV, iliyokuwa ikiendeshwa na Dk Dugange akiwa peke yake.
“Kutokana na mazingira hayo, THBUB imebaini kuwa kifo cha Nusura hakikuwa na uhusiano wowote na ajali ya gari ya Dk Dugange iliyotokea usiku wa Aprili 25, 2023,” inaeleza.
Hata hivyo, THBUB haikuthibitisha yeyote kuhusika na kifo cha Nusura kutokana na vielelezo vya Hospitali ya Faraja, Mkemia Mkuu wa Serikali na maelezo ya mengine ya mashahidi.
Tume hiyo imependekeza Jeshi la Polisi na mamlaka nyingine zichukue hatua kuwabaini wanaohusika na kutoa taarifa za uongo na chonganishi zinazosababisha taharuki katika jamii.
Imetaka jeshi hilo kwa kushirikiana na mamlaka za usafiri barabarani liweke vifaa vya kiusalama barabarani kama kamera ili kubaini matukio yanayotokea.
Iliwataka wananchi waepuke kutoa taarifa zinazochochea chuki na kusababisha uvunjifu wa amani.
Pia, iliwataka wananchi kuendelea kuwa na imani na vyombo vya dola katika kuzuia na kupambana na uhalifu na watoe ushirikiano katika kuvisaidia vyombo hivyo kutekeleza majukumu kwa ufanisi. |
Wakati safari ya Watanzania kwenda kupata Katiba mpya ikiendelea, Balozi Willibrod Slaa ameibuka na | Wakati safari ya Watanzania kwenda kupata Katiba mpya ikiendelea, Balozi Willibrod Slaa ameibuka na kukosoa vikali mchakato huo akisema kinachofanyika ni kiini macho na hauna uhalali kisheria.
Hoja ya mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, inatokana na alichoelezwa kuwa Katiba haipaswi kutungwa kwa maagizo ya Rais bali ni wananchi wenyewe.
Kauli ya Dk Slaa inakuja kipindi ambacho, Rais Samia Suluhu Hassan Mei 6, mwaka huu amemwagiza Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kuitisha baraza la vyama vya siasa kujadili mchakato huo.
Hata hivyo, kulingana na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Juma Khatibu mkutano huo utakaohusisha wadau mbalimbali utafanyika Agosti mwaka huu.
Hatua ya Rais Samia kutoa maagizo kwa Jaji Mutungi kuitisha baraza hilo, ndiyo iliyokosolewa zaidi na Dk Slaa akisema si misingi ya mchakato wa Katiba Mpya na Msajili hana mamlaka ya kutunga Katiba.
Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi nyumbani kwake jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alihusisha kinachofanyika sawa na kiini macho.
Mchakato unaofanyika sasa hasa kwa Rais Samia kumwagiza Jaji Mutungi katika mchakato huo, kwa mujibu wa Dk Slaa ni kiini macho.
"Hiki ni kiini macho na hakikubaliki kwa sababu maamuzi kuhusu Katiba na mabadiliko yake yanapaswa kuwa ya Watanzania na si kauli ya Rais au mtu mmoja," alisema.
Aliifananisha Katiba na mkataba wa ajira, akifafanua unapaswa kuandaliwa na mwajiri ambao ni wananchi kwa muajiriwa wao ambaye ni Rais na si mkuu wa nchi kuandaa.
"Sheria zinasainiwa na Rais, kwenye Katiba kuna sehemu ya saini ya Raia? Lakini hiki kiini macho eti Rais anaagiza Msajili itisha Baraza la vyama hakikubaliki," alisema.
Kinachopaswa kufanyika kwa mujibu wa Dk Slaa, ni kutungwa kwa sheria ya mabadiliko ya Katiba itakayoeleza mchakato mzima unavyopaswa kuwa.
Hilo lifuatiwe na kile alichoelezwa kuwa, mkutano wa wananchi wote kupitia vyombo vyao, wapendekeze utaratibu wa kuuendea mchakato na wanachohitaji katika Katiba hiyo.
"Mimi siamini kwamba hawajui mchakato unavyopaswa kuwa, siamini kwamba hawajui kuwa nchi inaongozwa kwa sheria na wameapa kwenye viapo vyao," alisema.
Mwanasiasa huyo aliyeziaga siasa za ndani ya vyama, alieleza kushangazwa na mchakato wa Katiba Mpya kupewa vyama visivyowahi kushinda katika chaguzi hata za Serikali a Mitaa.
"Hawana mtaa hata mmoja unawapa kazi ya kutengeneza Katiba, ndiyo hivi hivi kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 vyama karibu 14 vilijitokeza kudai eti uchaguzi ulikuwa huru na haki," alieleza.
Alihusisha kinachofanyika sasa na mwendelezo wa kuchafua chaguzi zinazotarajiwa siku zijazo kama ilivyokuwa mwaka 2020.
Kwanini inahitajika Katiba Mpya
DK Slaa aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania katika Nchi za Nordic, alisema haja ya Katiba Mpya inatokana na iliyopo kuwa katika mrengo wa siasa za chama kimoja.
Alisema Katiba iliyopo sasa ilitungwa na watu 20 akiwemo Thabit Kombo aliyekuwa Mwenyekiti na Pius Msekwa Katibu na wengine 18 ambao walianza kwa kuandaa ya CCM.
"Walipomaliza ya CCM wakaambiwa sasa tunataka mtutengenezee ya Serikali, ukitaka kujua kwa nini tunahitaji Katiba Mpya lazima ujiulize mbona ya CCM tangu 1977 imebadilishwa mara ngapi?" alisema.
Alihoji kwanini ya CCM imebadilishwa mara kadhaa lakini ya taifa isibadilishwe.
Jambo lingine linaloibua haja ya Katiba Mpya alisema ni hatua ya Mkuu wa nchi kuwa na mamlaka makubwa mithiri ya Mfalme.
"Leo Rais hapa ni kila kitu, Tanzania Rais ni Mungu, kama Mfalme hata nchi zenye mamlaka ya Malkia zimeshaacha, sasa sisi Tanzania tumerudi huko," alisema.
Kinachohitajika kwa mujibu wa Dk Slaa, ni Katiba itakayowapatia wananchi haki zao.
Msajili afafanua
Alipoulizwa kuhusu hilo, Jaji Mutungi alisema Msajili wa Vyama ni Katibu wa Baraza la Vyama vya Siasa na wajibu wake ni kuwezesha vikao vya Baraza la Vya Baraza la vyama vya Siasa.
"Ndugu mwandishi, nimeona concern yako, si vyema kama wengi wanavyojaribu kuupotosha umma.
"Kikosi Kazi ni matokeo ya mkutano wa wadau wa siasa ambao uliandaliwa na Baraza la Vyama vya Siasa, baraza lina haki ya kupokea mrejesho kuhusu mapendezo ya Kikosi Kazi," alisema.
Alisema: "Kwa kuwa sote tunatambua kwamba suala la Katiba ni la wananchi wote, ndiyo maana kwa agizo la Rais sasa baraza linaandaa mkuatano wa wadau ili kuona namna bora ya kuanza utekelezaji wa mchakato."
Hata hivyo, Jaji Mutungi alisisitiza hakupewa jukumu la kutunga Katiba na wala si kazi anayoifanya.
Anachokifanya, alisema ni uwezeshaji wa kuelekea mchakato wa utungwaji wa Katiba Mpya na ukifika wakati huo wenye mamlaka ya kufanya hivyo watapewa kutekeleza.
"Itafika hatua wenyewe wanaopaswa kutunga au kuandaa Katiba Mpya wataachiwa hiyo kazi waifanye, mimi nafanya uwezeshaji kuelekea mchakato huo situngi Katiba wala Sijapewa jukumu hilo," alisema.
Kwa sababu hizo hizo, alisema ndiyo maana amewaambia hata wanasiasa wasibweteke wakiamini kwamba wao ndiyo pekee wenye mamlaka ya kuandaa Katiba Mpya hapana, ni jukumu la wananchi wote.
"Ingawa nipo Uturuki kwa matibabu mlipaswa kunipumzisha lakini nimelazimika kulijibu hili ili ieleweke vema," alieleza.
Simu ya Waziri wa Katiba na Sheria, iliita bila majibu, huku Naibu wake akijibu kwamba yupo bungeni hivyo asingeweza kuongea.
CCM kukagua miradi
Mbali na hoja kuhusu Katiba Mpya, Dk Slaa alieleza kushangazwa na hatua ya CCM kukagua miradi na hata kutoa maagizo kwa mamlaka za Serikali.
Alisema hiyo ni kazi ya vyombo vya Serikali na si CCM, akisisitiza ikihitaji kufanya hivyo inapaswa kuandika kwa mamlaka husika ya Serikali.
"Juzi nimeona Katibu Mkuu wa CCM (Daniel Chongolo) anaagiza kuchomwa barabara na kesho yake trekta limekwenda, hivi bajeti inatoka wapi," alisema.
Alisema CCM haina bajeti ya kutekeleza miradi ya Serikali inapata wapi mamlaka ya kuagiza na utekelezaji ufanyike.
Mambo hayo, alieleza ndiyo yanayofanya nchi iongozwe kiholela.
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Katibu Mkuu 2q CCM, Daniel Chongolo simu yake iliita bila majibu.
Hali ilikuwa hivyo hivyo hata kwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema.
Makali yake akiwa nje ya Serikali
DK Slaa alisema so kweli kama inavyodhaniwa na wengi kwamba alikuwa kimya juu ya kuikosoa Serikali alipokuwa mtandaji wa umma.
"Nilikuwa Balozi na nilikuwa na nafasi ya kuhojiana na Rais moja kwa moja, asikilize asisikilize shauri yake lakini mimi ushauri umefika.
"Sasa natoka hadharani kufanya nini wakati nina nafasi ya kumwambia Rais moja kwa moja, ndiyo maana hata Mawaziri huwasikii wakiongea," alisema.
Alieleza maneno yake hayahusiani na hasira ya kuwa nje ya mfumo wa Serikali kwa kuwa kwanza ana umri wa kustaafu miaka 74, pia ni Mwenyekiti wa CCBRT ambayo ina bajeti kubwa inayokaribia ya Wizara.
"Tangu nianzishe taasisi sijachukua hata senti tano, hata nikienda hata ya mafuta sichukui sasa serikalini natafuta nini, wenye mawazo hayo kichwani wana njaa," alisema.
Kuhusu Chadema
Kwa mujibu wa Dk Slaa, hapendelei kuikosoa Chadema kwa kile kinachoaminiwa na wengi kuwa akifanya hivyo ni kwa sababu ana hasira nayo.
Alipoulizwa iwapo itawezekana kwake kurejea ndani ya chama hicho, alisema hana mpango huo kwa kuwa aliapa kufanya siasa ndani ya vyama vya siasa.
Kuondoka kwake ndani ya chama hicho, kilitokana na kile alichoeleza kuwa walioleta choo sebuleni, ingawa halipo tena alishaapa kutofanya siasa ndani ya vyama.
"Nikishasema mwanasiasa makini akitoa kiapo huwa habadiliki, mimi niliapa najitoa kwenye siasa ya vyama na nikarudia lakini ninapoona nchi yangu inaenda vibaya nitaendelea kupiga kelele nitaongea kama raia," alisema.
Elimu bila malipo
DK Slaa alisema sera ya elimu bure inayotekelezwa na CCM chimbuko lake ni Chadema, hata hivyo haitekelezwi kama walivyotarajia.
"Mimi naamini Chadema wakati ule tungeshinda tungetekeleza vizuri tena tungetoa elimu bora.
"Hatulalamiki kwa CCM kuitekeleza kwa sababu ilani ya chama cha siasa ni mali ya wananchi, ukizungumza kesho aliyeshinda uchaguzi akichukua sio ameiba," alisema.
Kwa wakati huo, alisema ingewezekana kwa Chadema kutekeleza sera hiyo hadi ngazi ya elimu ya juu.
Nafasi ya upinzani kushika dola
Kwa mujibu wa Dk Slaa, wingi wa vyama nchini hauna tofauti na Congo ya Mobutu Sseseseko aliyetengeneza vyama 2,000 vya siasa vya kushindia uchaguzi.
Lakini, alisema kuna nafasi ya ushindi kwa vyama vya upinzani siku za karibuni kwa kuwa utafika wakati wananchi wataelewa na kukataa kinachofanywa na Serikali.
"Ukimbinya mtu sana hata yule ambaye alikuwa haelewi ataelewa na atakataa, kwa hiyo Serikali itafika mahali itabadilika tu ndivyo ilivyo katika historia ya nchi nyingi," alisema.
Anachofanya sasa
Mstaafu huyo kwa sasa alisema anajishughulisha na uandishi wa vitabu kazi ambayo aliianza tangu miaka 50 iliyopita.
Mbali na uandishi wa vitabu, alieleza utafiti wa mambo mbalimbali hasa ya siasa ni shughuli nyingine anayojishughulisha nayo kwa sasa.
"Kwa sasa nafanya utafiti zaidi katika siasa, naangalia mfumo wa vyama vingi katika Afrika Mashariki lakini mtarajie vitabu," alisema.
Kuhusu ukatili
Alisema kutengenezwa mazingira mazuri ikiwemo kutoa mshahara utakaowatosheleza watu ndiyo jambo pekee litakalopunguza vitendo hivyo.
Alisema vitendo hivyo kwa kiasi kikubwa vinachagizwa na watu kushindwa kuzihudumia familia zao. |
Sakata la uraia pacha limeendelea kuwa kitendawili kisichoteguka, baada ya diaspora kulalamikia kuto | Sakata la uraia pacha limeendelea kuwa kitendawili kisichoteguka, baada ya diaspora kulalamikia kutoshirikishwa katika uamuzi wa Serikali wa kutoa hadhi maalum kwa raia hao wanaoishi nje ya nchi.
Uamuzi wa Serikali kutoa hadhi maalum kwa diaspora badala ya uraia pacha, ulitangazwa juzi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax.
Katika hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2023/24, Dk Tax alisema: “wizara ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuwapatia Hadhi Maalum Diaspora wenye asili ya Tanzania na uraia wa nchi nyingine.”
Licha ya Serikali kueleza kuwa imeshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo diaspora katika uamuzi huo, raia hao wanaoishi nje ya nchi wameonyesha upinzani wakisema hawakushirikishwa.
Hilo linasisitizwa na Balozi wa zamani wa nchi za Nordic, Willibrod Slaa aliyesema upinzani unaoibuka unatokana na kutoshirikishwa kwa diaspora katika mchakato huo.
Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi nyumbani kwake jijini Dar es Salaam, Balozi Slaa alisema malalamiko ya diaspora kwenye mchakato wa kutoa hadhi maalum ni kutoshirikishwa kwao.
Hilo linathibitishwa na kile alichokieleza kuwa, pamoja na Serikali kutoa hadhi maalum haieleweki kuna nini ndani yake akihoji zaidi: “Kuna mtu anajua, Serikali iliwashirikisha, iliwahoji?”.
“Kila kitu tunachofanya sisi ni mabavu mabavu, naamini watu wangeshirikishwa kusingekuwa na kelele zinazopigwa sasa,” alisema.
Kilichopaswa kufanyika, Dk Slaa alipendekeza ni Serikali kujadiliana na watu wake, wapange pamoja, watafute njia rahisi itakayokubalika na wote na kuwalinda kwa uhakika.
“Tatizo naloliona Serikali haijajadiliana na watu wake haijataka kukaa chini na watu wake, matatizo mengine Serikali inajitafutia yenyewe kwa kutowashirikisha watu,” alisisitiza.
Mwanadiplomasia huyo aliyeiwakilisha Tanzania katika mataifa ya Denmark, Norway, Sweden, Finland na Iceland alisema wakati mwingine Serikali inashindwa kufikia malengo tarajiwa kwa kutojiandaa vizuri.
“Matatizo yapo kwetu tunashindwa kujiandaa vizuri kabla ya kufanya jambo tunalotaka kulifanya, nia inaweza kuwa njema lakini kwa kukosa umakini tunashindwa kufikia malengo tarajiwa,” alisema Dk Slaa.
Suala la uraia pacha, alisema halipaswi kuwa mjadala kwa kuwa waliokwenda nje ya nchi wamefuata kutafuta maisha na Serikali ilikiri faida iliyopatikana kutoka kwao.
“Serikali yenyewe imetamka kwamba kwa mwaka uliopita diaspora wameleta zaidi ya Sh2 trilioni. Duniani hakuna kitu chenye manufaa kama fedha zinazotoka kwa watu wanaoishi nje ya nchi,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk Slaa, safari ya watu kutoka katika mataifa yao kwenda kwingineko inatokana na nchi zao zimeshindwa kuwapatia mahitaji muhimu ikiwemo ajira.
“Mwananchi kupoteza uraia wa nchi yake, uraia amepewa na Mungu hii nyingine umeukana kwenye karatasi lakini babu na bibi yake wapo Tanzania, hata kama wamekufa lakini makaburi yao yapo hapa.
“Sasa unawaondoaje hawa ambao vitovu vyao vilizikwa hapa Tanzania, labda Serikali haijafanikiwa kujadiliana na raia wake ili kufikia muafaka unaotakiwa,” alisema.
Kinachoelezwa na Dk Slaa kinathibitishwa na raia wa Tanzania anayeishi nchini Uingereza, Tito Magoti aliyesema kumekuwa na uhaba wa mazungumzo kati ya Serikali na diaspora yaliyosababisha kukosekana kwa muafaka.
“Bahati mbaya Serikali inaona kwamba imewashirikisha na kuna watu hawakubaliana na hilo ilivyo ni kama Serikali ilikuwa na maoni yake na haikuhitaji ya watu wengine.
“Diaspora wanashangaa wanaambiwa wameshirikishwa wapi na lini,” alisema.
Hata hivyo, Magoti alisema mahitaji ya uraia pacha yanalenga kurahisisha upatikanaji wa huduma hususan kwa wananchi wazawa.
Lakini, hadhi maalum alisema inapora haki ya kuzaliwa na kwamba upembuzi unaoelezwa kuwa hilo ni jambo lenye manufaa zaidi ni maoni ya Serikali si diaspora wenyewe.
“Kama mataifa mengine hawana uraia pacha, isitumike kuwaadhibu watu wengine wanaohitaji kufurahia haki yao ya kuzaliwa katika taifa fulani,” alisema Magoti.
Mtazamo wa Magoti ni tofauti na Mwenyekiti wa Klabu ya Diaspora Tanzania (TDC), Kelvin Nyamori anayeunga mkono hatua inayotarajia kuchukuliwa na Serikali ya kutoa hadhi maalum kwa raia wake.
“Kuna watu wanataka kupinga, sisi kama diaspora wazalendo tunakubaliana na hadhi maalum kwa maslahi ya taifa, tunashukuru kwa hatua hii ya Serikali maana imeona ifanye jambo kwa ajili yetu,” alisema.
Alipoulizwa kuhusu kushirikishwa, alisema Serikali imefanya hivyo kupitia kwa taasisi zinazowaunganisha diaspora.
00000
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema hatua ya Tanzania kuhamia katika nishati safi ni miongoni mwa mambo muhimu katika ajenda ya taifa.
Kauli hiyo ya majaliwa inakuja siku moja baada ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kusaini mkataba wa Sh274.7 bilioni kwa ajili ya mradi wa umeme wa nishati ya jua Megawati 150 wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga.
Majaliwa alitoa kauli hiyo jana, katika hotuba yake katika maonyesho ya Nishati yaliyoandaliwa na Wizara ya Nishati.
Alisema Serikali imeunda kamati ya kitaifa kwa ajili ya kuongeza uelewa wa jamii na kuwaonyesha wajasiriamali fursa zitakazopatikana kutokana na nishati safi.
Kuundwa kwa kamati hiyo, alisema ni agizo za Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa Novemba mwaka jana ambalo pamoja na mambo mengine aliielekeza kupitia upya sera kuelekea kwenye mpango wa kitaifa wa kutokomeza nishati chafu ya kupikia mwaka 2032.
“Kwa kuanzia kama nchi, tutashinikiza matumizi ya nishati mbadala katika taasisi kubwa kama za elimu, kambi za jeshi, vyuo, na shule za sekondari,” alisema.
Mei 29, mwaka huu Tanesco ilisaini mkataba wa mradi wa umeme wa nishati ya jua, ikiwa ni juhudi za Serikali za kufikia maendeleo endelevu na kuwa nchi kiongozi katika ubunifu wa nishati jadidifu.
Kulingana na Meneja wa Miradi, Usafirishaji na Usambazaji kutoka Tanesco, Frank Mashalo mradi huo utaanza Juni mwaka huu na awamu ya kwanza itazalisha megawati 50 za umeme.
Alisema mradi huo utatekelezwa kwa muda wa mwaka mmoja na mkandarasi kutoka China, Sinohydro Corporation.
“Mradi huu unalenga kuongeza uhakika wa usambazaji nishati nchini na ni sehemu ya dhamira ya Tanesco kuhakikisha kunakuwa na mchanganyiko wa nishati kutoka vyanzo mbalimbali,” alisema.
Mashalo alisema mradi huo pia utachangia sehemu ya juhudi za kuhamia katika nishati safi.
Akizungumza wakati wa utiaji saini wa mkataba huo, Waziri wa Nishati, January Makamba alisema mradi huo ni mkubwa na pekee Afrika Mashariki.
Kuhusu mpango wa Serikali wa kuhamia katika nishati safi, Makamba alisema utafanikiwa iwapo kila kaya itatumia nishati safi kwa ajili ya kupikia.
“Nishati nyingi hazitumiki viwandani na kwenye vyombo vya usafiri. Kwa sehemu kubwa zinatoka katika kaya zetu na unapozungumzia kaya shughuli kubwa ni mapishi,” alisema.
Kwa mujibu wa Makamba, Tanzania inaendelea kuweka kipaumbele katika uwekezaji wa miundombinu ya nishati mbadala na inatarajia kufungua fursa nyingi za kiuchumi na mazingira.
Hata hivyo, alisema kuna ombwe kubwa la uelewa kuhusu nishati safi, jambo linalompa jukumu kila mmoja kuhakikisha wanajenga uelewa huo.
Ingawa zinatajwa kuwa nishati nafuu, mkaa, kuni na mabaki ya mazao ndizo zinazochangia vifo vingi vya watu nchini takwiban 33,000 kwa mwaka, kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Nishati.
Ni asilimia nane ya kaya ndizo zinazotumia nishati safi ya kupikia nchini, huku Kenya ikiwa ni asilimia 17, wakati wastani wa dunia ni angalau asilimia 70. Hata hivyo, asilimia 80 ya kaya nchini hutumia kuni, mkaa na mabaki ya mazao kama chanzo cha nishati ya kupikia.
Takwimu za Waziri Makamba, zinabainisha kuwa mtu anayekaa kwenye moshi wa jiko la kuni kwa saa ni sawa na kuvuta sigara 200 hadi 300. |
null | ### Contact Us
##### Contacts Us
**Postal Address**
The United Republic of Tanzania
Ministry of Finance
Treasury Square Building 18 Jakaya Kikwete Road
P.O.BOX 2802,
40468 Dodoma.
40468 Dodoma. |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | Copyright © 2014 - 2024 e-Government Authority. All Rights Reserved | GMS Version 4.0.0
Warning: This webmail service requires Javascript! In order to use it please enable Javascript in your browser's settings. |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | null |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | About
Press
Copyright
Contact us
Creator
Advertise
Developers
Terms
Privacy
Policy & Safety
How YouTube works
Test new features
© 2024 Google LLC |
null | |
null | null |
null | |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
null | - Mwanzo
- Utawala
- Kuhusu Sisi
- Mikoa
-
Miradi
- Tanzania Strategic Cities Project
- MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
- Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
- v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
- Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
- Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
- UNFPA
- Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
- Msimbazi Basin Development Project
- Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
- Primary school Development Plan
- Secondary school Development Plan
- Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
- Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
- Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
- Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
- Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
- Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
- LIC
- Program (PFMRP)
- Rural - Urban window
- Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
- Kituo cha Habari
- Vijiji na Miji
- Nyaraka
- Mifumo
- Maktaba ya Video |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.