text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
HASSAN DAUDI NA MITANDAO ANAITWA Andre
Rush, umri wake ni miaka 45. Ni wananchi wachache wa Marekani wasiomfahamu huyu
jamaa. Licha ya
umaarufu alionao, majukumu yake ya kazi huishia jikoni tu. Hicho ndicho
kilichomweka ndani ya Ikulu ya Marekani, kuhakikisha milo mitatu inapatikana,
tena kwa wakati, kwa kila mfanyakazi. Ni tofauti na
wafanyakazi wengine wa Ikulu ya nchi hiyo, ambao aghalabu utawaona katika kila
msafara wa Rais Donald Trump. Rush
ataonekana hadharani siku za sherehe na hafla zingine, jukumu lake kubwa likiwa
ni kuandaa keki au msosi ‘uliokwenda shule’ kwa maofisa na wageni
waliohudhuria. Katika siku za
kawaida, utamkuta jikoni, akihusika kwa kila hatua ya chakula anachokula Rais
Trump na watu wengine ndani ya Ikulu. Hiyo
inamaanisha ana ratiba ya chakula ya kila siku, anatakiwa kusimamia ubora wa
mlo wenyewe, kwa maana ya usalama wa kiafya na zaidi ya hapo, aingie jikoni
kuanza kukarangiza. Jamaa amekuwa
akiifanya kazi hiyo ya kuwapikia wakubwa Ikulu ya Marekani tangu mwaka 1997,
ikimaanisha kuwa si Rais Trump pekee, bali amewahudumia viongozi wote
waliopita, wakiwamo George W. Bush na kipenzi cha Waafrika, Barack Obama. Wasifu wa Rush
unamtaja kuwa ni sajenti mstaafu na alilitumikia Jeshi la Marekani kwa miaka
24, kabla ya kugeukia shughuli ya kuandaa madikodiko. Kwa mara ya
kwanza, baada ya kustaafu utumishi wake jeshini, Rush alijitosa katika upishi
mwaka 1994 na moja kati ya matukio yaliyompa jina ni lile la kutengeneza keki
yenye urefu wa futi 16. Lakini pia, baba
huyo wa watoto wanne amejijengea umaarufu mkubwa kutokana na mwonekano wake wa
kuvutia unaotokana na mazoezi ya kutanua misuli. Hata umaarufu
wake uliongezeka mara dufu Juni, mwaka jana, baada ya mkono wake uliojengeka
kimazoezi kuonekana na kuwavutia wengi. Siku hiyo alikuwa katika majukumu yake
ya upishi. Akilizungumzia
hilo la mwili wake mkubwa unaoweza kuufananisha na waigizaji wa filamu za
mapigano kama Arnold Schwarzenegger, anasema: “Kuna kipindi
Rais Bush alinipongeza kwa jinsi nilivyo fiti na aliniuliza huwa nafanya nini
kuwa hivi. Hata Rais Obama na viongozi wengine wakubwa wamekuwa wakiniuliza.
Ninachowaambia ni kujitoa kwa kwenda mazoezini (gym). Hakuna zaidi ya hapo. “Huwa napiga
‘pushapu’ 2,222 kila siku na nilianza kufanya hivyo ikiwa ni kampeni ya
kuwakumbuka maveterani wa kijeshi 22 wanaopoteza maisha kila siku kwa kujiua,”
anasema. Katika mahojiano yake na jarida la afya la men’s health, Rush anasema katika idadi hiyo, huwa anapumzika dakika tatu tu, zikizidi sana 10, kila anapofikisha 200. Aidha, haishii
katika pushapu, bali ili kujiweka fiti zaidi, amekuwa akihudhuria mara kwa mara
vituo vya mazoezi (gym). “Huwa nakwenda
gym kila siku na huko natumia saa moja au mbili hivi,” anasimulia Rush na
kuongeza: “Kutokana na mazoezi makali hayo, huwa nakula chakula kingi.” Akiliambia jerida hilo la men’s health nasema asubuhi pekee huwa inakaa poa endapo anapata mayai ya kuchemsha 12 au 24 na maziwa. Si kwamba
mchana utapita hivi hivi, lazima msomi huyo wa shahada ya uongozi wa biashara
apate kuku wanne wa kukaanga ili mambo yaende sawa katika majukumu yake ya kazi
za jikoni, huku akisubiri chakula cha usiku, ambacho huenda akarudia kama
mchana au akabadilisha. Mbali ya majukumu yake, Rush amekuwa mstari wa mbele katika
kampeni ya kuwasaidia maveterani wa jeshi, ambao kwa Marekani wamekuwa
wakiripotiwa kukabiliwa na msongo wa mawazo unaosababisha wajiue. Hivyo basi, alichoamua kukifanya mpishi huyo ni kuandika
kitabu cha vyakula kiitwacho ‘Combat Food Medic’, akitazamia kutoa elimu ya
milo inayoweza kupunguza kiwango cha msongo wa mawazo. “Kupika kulikuwa na msaada mkubwa kwangu katika tiba (dhidi
ya msongo wa mawazo),” anasema Rush kuliambia jarida la Men’s Health. Kuhusu familia yake anasema: “Watoto wangu nao wako
fiti pia… Nawafundisha namna ya kupika vyakula vyenye afya…” | 2 |
SERIKALI ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo la Kimataifa (JICA) inakusudia kuipatia Tanzania mkopo nafuu na ruzuku wenye thamani ya zaidi ya dola milioni 345 za Marekani, sawa na takriban Sh bilioni 794, kwa ajili ya kutekeleza miradi mitatu ya maendeleo.Miradi hiyo ni ukarabati wa barabara ya Arusha hadi Holili, ukarabati wa Bandari ya Kigoma na Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Visiwani Zanzibar. Ahadi hiyo ilitolewa na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la JICA anayesimamia Ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara Hiroshi Kato, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, mjini Washington D.C nchini Marekani. Aliitaja miradi hiyo iliyoko mezani kwao inayosubiri kupatiwa fedha wakati wowote kuanzia sasa kuwa ni pamoja na mradi wa ukarabati wa barabara ya Arusha-Holili utakaopatiwa mkopo wa dola milioni 221.Aliutaja mradi wa pili kuwa ni wa majisafi na usafi wa mazingira Zanzibar utakaopatiwa fedha kupitia mkopo wa dola milioni 99 na mradi wa upanuzi wa Bandari ya Kigoma ambao Japan itatoa ruzuku ya dola za Marekani milioni 25. Kato alisema kuwa Japan inajivunia ushirikiano wa muda mrefu kati yake na Tanzania na kwamba iko tayari kusaidia juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano za kuwaletea wananchi wake maendeleo na kuitaka serikali kuwasilisha miradi yake ya kimkakati ambayo Japan itafadhili kupitia mikopo yenye riba nafuu pamoja na ruzuku. | 3 |
ZIARA ya siku mbili nchini Namibia ya Rais, Dk John Magufuli imeelezwa kuanza kuonesha mafanikio baada ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupokea ugeni kutoka Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomiliki kiwanda cha kuchakata nyama nchini humo iliyoonesha nia ya kuwekeza hapa nchini.Hayo yalithibitishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel ambaye amemshukuru Rais Magufuli kutokana na ziara yake ya kikazi ya siku mbili aliyofanya nchini Namibia kuanzia Mei 27 hadi 28 mwaka huu.Akizungumza ofisini kwake jijini Dodoma na mmoja wa wakurugenzi katika kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd Hendrick Boshoff, Profesa Gabriel alisema lengo la ziara yake ni kupata taarifa za awali, kutoka kwa wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili waweze kuwa na njia sahihi ya uwekezaji ambao utakuwa na tija kwa watanzania kupitia sekta ya Mifugo.“Mheshimiwa rais alifanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Namibia akiambatana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina na viongozi wengine, nichukue fursa hii kwa niaba ya wizara kumshukuru mheshimiwa rais kutuanzishia suala la soko la mazao ya mifugo hususan nyama, tumetembelewa na mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomiliki kiwanda cha kuchakata nyama nchini Namibia ili kukutana na wataalam baada ya rais kuonesha muelekeo na wao wakaitikia,” alisema Profesa Gabriel.Katika mazungumzo hayo Katibu Mkuu huyo aliuhakikishia ugeni huo kutoka Namibia kuwa wizara iko tayari kuhakikisha nia ya kampuni hiyo kuanzisha kiwanda kingine cha kuchakata nyama hapa nchini inafikia katika utekelezaji baada ya ziara ya mheshimiwa rais nchini Namibia. Profesa Gabriel alieleza kuwa ujio wa ugeni huo unaratibiwa na wizara nne zikiwemo za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Viwanda na Biashara, Ofisi ya Waziri Mkuu eneo la Uwekezaji na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Sekta ya Mifugo.Aidha, ametoa wito kwa watanzania kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali hususani zinazolenga kuongeza masoko ya kutengeneza na kuuza bidhaa zinazozalishwa hapa nchini. “Viwanda kama hivi vikija ajira nyingi zitaongezeka na pia pato la taifa litaongezeka, bado tuko chini katika ulaji wa nyama takwimu zilizotolewa na Shirika la Chakula Duniani (FAO) zinaonesha walau mtu wa kawaida anatakiwa kula kilogramu 50 kwa mwaka, bado kwa watanzania tunakula kilogramu 15 kwa mwaka mzima, tunaleta wenzetu waongeze bidii katika hilo ili wazalishe na soko la ndani liwepo tuuze na nje ya nchi,” alifafanua Profesa Gabriel.Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomikili kiwanda cha kuchakata nyama nchini Namibia Hendrick Boshoff alimwambia Profesa Gabriel kuwa, kampuni hiyo ilianza kuendesha shughuli zake miaka 40 iliyopita na wamekuja nchini Tanzania wakilenga zaidi uwekezaji wa kuyaongezea thamani mazao ya mifugo hususan nyama.Akimuakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Viwanda Vidogo na Kati (DSME), Dk Consolata Ishebabi alisema ugeni huo utafahamishwa pia fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) ili kufahamu mazingira mbalimbali ya uwekezaji yakiwemo ya sekta binafsi.Aidha, Dk Ishebabi alifafanua kuwa ugeni huo utafikishwa pia katika Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) ambapo watafikishwa katika Ranchi ya Kongwa ambayo ipo chini ya NARCO kuweza kuona aina ya mifugo iliyopo nchini na waweze kupata taarifa za jumla ambazo zitawapatia mwanzo mzuri wa kuwekeza hapa nchini katika Sekta ya Mifugo. | 3 |
Na MWANDISHI WETU-ARUSHA MHADHIRI Msaidizi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, Haliye Mabakwe
(32),amepandishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na kusomewa mashtaka mawili,
likiwemo la kuomba rushwa ya Sh 450,000 kwa wanafunzi ili awafaulishe katika
mitihani ya marudio. Jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo,Martha
Mahumbuga,Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU),Richard
Jacopiyo, alidai kosa la kwanza, ni mshtakiwa
kujihusisha na vitendo vya rushwa kati ya Septemba 9 na 15, mwaka huu,
akiwa eneo la Tengeru chuoni hapo. “Mshtakiwa akiwa mwajiriwa wa chuo, aliomba rushwa ya
shilingi 450,000 kutoka kwa mwanafunzi Joyce Deogratias ambaye alikuwa
akikusanya na za wanafunzi wenzake wane wanaosoma chuoni hapo ili awasaidie
kufaulu mitihani yao (Supplementary Exams),”alidai Alidai shtakala la pili
ni kujihusisha na vitendo vya rushwa, ambapo kati ya Septemba 9 hadi 15, mwaka huu alipokea rushwa ya Sh 449,000 kutoka
kwa Joyce za wanafunzi wanne kwa lengo
la kuwafaulisha kwenye masomo yao waliyofeli. Mshtakiwa alikana
mashtaka hayo, huku Wakili Jacopiyo akiomba mahakama kuahirisha shauri hilo kutokana
na upelelezi wake kutokamilika. Mshtakiwa aliachiwa
kwa dhamana na Hakimu Mahumbuga kuahirisha kesi hiyo hadi Januari 8, 2020,
itakapotajwa tena. Awali taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mkuu wa
Takukuru mkoani hapa,Frida Wikesi ilidai
mshtakiwa alikuwa akiwashawishi
wanafunzi wake wa astashahada mwaka wa mwisho kumpatia rushwa ya fedha ili
awafaulishe katika somo la Participatory Research Methods,ambalo yeye hufundisha. “Uchunguzi wa Takukuru, umebaini mtuhumiwa alikuwa akiwaomba shilingi 50,000 kila
mwanafunzi ambaye hakufaulu katika mitihani ya somo hilo,ushawishi aliokuwa
akiufanya kupitia mwanafunzi huyo ambaye alikuwa akipokea fedha hizo kwa
wanafunzi wenzake na kuzituma kwa mwalimu huyo kwa miamala ya simu na
benki,”ilidai taarifa hiyo | 3 |
HALI ya uchumi nchini imeendelea kuimarika ambapo kwa mwaka 2018 pato halisi la taifa lilikua kwa asilimia 7.0 na hivyo Tanzania kushika nafasi ya pili kwa ukuaji uchumi kwa nchi za Afrika Mashariki, huku Rwanda ikishika nafasi ya kwanza kwa uchumi wake kukua kwa asilimia 8.6.Halikadhalika, nchi ya Kenya imeshika nafasi ya tatu kwa ukuaji uchumi kwa nchi za ukanda huo ambapo uchumi wake umekua kwa asilimia 6.3 ikifuatiwa na Uganda ambayo uchumi wake umekua kwa asilimia 6.1.Akiwasilisha taarifa ya hali ya uchumi wa Taifa katika mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2019/20 bungeni jana, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema ukuaji wa uchumi wa Tanzania umechochewa zaidi na kuongezeka kwa uwekezaji hususani katika miundombinu mbalimbali.Kiasi cha fedha kilichotengwa na serikali kugharamia Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2019/20 ni Sh trilioni 12.24, fedha za ndani kati ya hizo, ni Sh trilioni 9.73 na fedha za nje ni Sh trilioni 2.51.Aidha fedha hizo za maendeleo ni sawa na asilimia 37 ya bajeti yote ya mwaka 2019/20.Aliitaja miundombinu hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa reli, barabara na viwanja vya ndege, kuimarika kwa huduma za usafirishaji huku sekta ya kilimo ikitoa mchango mkubwa kwa asilimia 28.2Akizungumzia ukuaji wa uchumi wa nchi, Dk Mpango alisema kwa mujibu wa takwimu mpya za mwaka wa kisio wa 2015, pato halisi la Taifa lilikua kwa asilimia 7.0 mwaka 2018 ukilinganisha na ukuaji wa asilimia 6.8 kwa mwaka 2017.Alisema pamoja na hali ya uchumi wa dunia kupungua kwa kasi ya ukuaji kutoka asilimia 3.8 ya mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 3.6 kwa mwaka 2018 kutokana na kupungua kwa mahitaji ya bidhaa na huduma kutoka nje na hali ya wasiwasi kuhusu madhara ya Uingereza kujitoa Jumuiya ya Ulaya, bado uchumi kwa nchi za Afrika Mashariki uliimarika zaidi.“Mwenendo wa Uchumi wa Nchi za Afrika Mashariki ulikua ambapo Rwanda, uchumi wao ulikua kwa asilimia 8.6 mwaka 2018 ukilinganisha na asilimia 6.1 mwaka 2017, Tanzania ilikua kwa asilimia 7.0 mwaka 2018 ukilinganisha na asilimia 6.8 mwaka 2017, Kenya wao uchumi wao ulikua kwa asilimia 6.3 ukilinganisha na asilimia 4.9 mwaka 2017,Uganda uchumi wao ulikua kwa asilimia 6.1 mwaka 2018 ukilinganisha na asilimia 5.9 mwaka 2017,”alisema Dk Mpango.Alisema mbali na ukuaji huo wa uchumi, Dk Mpango alisema Tanzania Bara inakadiriwa kuwa na watu milioni 52.6 na kwamba wastani wa pato kwa mtu wa kawaida kwa mwaka lilikuwa Sh milioni 2.45 ambacho ni sawa na dola za Marekani 1,090 ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.4 kwa mwaka 2017.Akizungumzia mwenendo wa bei, Dk Mpango alisema mwaka 2018 mfumuko wa bei uliendelea kubaki katika wigo wa tarakimu moja na kufikia kiwango cha chini kabisa kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka 40 iliyopita.Alisema katika kipindi hicho cha mwaka 2018 mfumuko ulipungua kutoka wastani wa asilimia 5.3 mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 3.5 mwaka 2018 na hadi Aprili mwaka huu mfumuko wa bei ulikuwa asilimia 3.2 ukilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2018.Dk Mpango alisema mfumuko huo wa bei wa chini ulitokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuimarika kwa hali ya upatikanaji wa chakula katika masoko ya ndani na nchi jirani na uzalishaji wa chakula ulifikia tani milioni 15.9 ikilinganishwa na mahitaji ya tani milioni 13.3 kwa kipindi hicho. | 5 |
Shein kauli hiyo aliitoa jana mara baada ya kuchukuwa fomu ya kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar baada ya waandishi wa habari kutaka kujua msimamo wa Serikali na mgogoro wa chama hicho ambao sasa umegonga hodi mahakamani.Alisema kuwa hatua ya mambo ya michezo kuyapeleka mahakamani haileti taswira nzuri na wala haitengenezi na badala yake inazidisha kuzorotesha mchezo huo.Alisema kuwa Zanzibar iliweza kung’ara katika miaka ya nyuma katika Afrika Mashariki, lakini sasa wamekuwa nyuma jambo ambalo halitoweza kurejea kwa hatua hii waliyofikia.“Tuling’ara sana katika miaka ya nyuma katika Afrika Mashariki lakini kwa hatua hii tuliyofikia hatuwezi kung’ara, kwani unapokwenda mahakamani usifikirie unatengeneza bali unaharibu kwani mipangilio ya kimahakama unachukuwa muda mrefu na inazuia shughuli zenu za kuimarisha michezo”, alisema Dk Shein.Hata hivyo, alisema kuwa akiwa rais wa nchi anaiheshimu sana sheria za FIFA ambazo zinakataza Mamlaka za Serikali kuingilia mambo ya soka kwa wanachama wake na kusema kuwa yuko tayari kushirikiana katika kuendeleza mchezo huo.“Mimi sina tatizo kushirikiana katika kuendeleza mchezo huu, tatizo lipo kwa viongozi na wadau wa michezo ambao wanashindwa kufanya kazi pamoja kwa maendeleo ya soka na musifikirie kwa hatua hii kwamba tutafanikiwa”, alisema.Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) Taifa kimeshinda kufanya uchaguzi Mkuu baada ya viongozi wake wakuu kushitakiana mahakamani akiwemo Makamu wa Rais, Haji Ameir kuwashitaki rais wa chama hicho Ravia Idarous Faina na makamu wa rais Pemba, Ali Mohammed kwa kuwahusisha na matumizi mabaya ya fedha pamoja na kukubali kupitisha katiba ya chama hicho ambayo inakwenda kinyume na sheria za mchezo huo.Kujitokeza suala hilo umepelekea pia waliokuwa wakidhamini Ligi Kuu ya Zanzibar, Grand Malt kushindwa kuendelea na udhamini huo kwa madai ya kukosa raha ya kusumbuliwa na askari polisi ambao wamekuwa wakifika ofisini kwao kuwahoji. | 4 |
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Tanga (Takukuru) imetoa onyo kwa wagombea uongozi katika nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani ambao watajitoa dakika za mwisho.Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga, Christopher Mariba alitangaza kiama kwa wagombea hao wakati akitoa taarifa ya taasisi hiyo ya mwezi Julai hadi Septemba mwaka huu kwa Mkoa wa Tanga alipozungumza na waandishi wa habari hapa. Mariba alielezea mikakati ya taasisi hiyo kuelekea uchaguzi zijazo itafanyia kazi mambo ambayo chaguzi za awali zilizopita yalikuwa yakifanywa kiholela na kinyume cha sheria.Kwenye chaguzi za serikali za mitaa Novemba 24 mwaka huu na mwaka 2020 hatutakuwa na mgombea atakayejitoa dakika za mwisho na atakayefanya hivyo hatua kali zitachukuliwa kwake.Kuhusu miradi, Mariba alisema miradi 33 ya maendeleo yenye thamani ya sh 7842,182,458.76 sekta ya elimu inayotekelezwa mkoani Tanga na kubaini baadhi yake ina dosari mbalimbali. Miongoni mwa dosari ambazo Takukuru imezibaini ni udokozi mkubwa wa fedha za ruzuku zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kupeleka kwenye shule za Halmashauri za Mkoa wa Tanga.Alisema katika ufuatiliaji huo,Takukuru imebaini kuwepo kwa ukiukwaji taratibu za manunuzi kwa baadhi ya miradi ya ukarabati majengo ya Serikali hasa shule na ununuzi wa vifaa kwa matumizi ya shule na maeneo mengine hakuna uwazi. | 3 |
BERLIN, UJERMANI KANSELA Angela Merkel, ametoa wito wa kutafakari upya mtazamo wa Serikali ya Ujerumani kwa Uturuki baada ya taifa hilo kuwakamata raia wao wawili zaidi. Uhusiano kati ya nchi hizo mbili umelegelega tangu jaribio lililoshindwa la mapinduzi mwaka 2016. “Hakuna msingi wa kisheria wa kukamatwa kwao,” alisema Merkel akielezea kuhusu Wajerumani hao waliokamatwa Alhamisi iliyopita nchini Uturuki. Kukamatwa kwao kunafikisha idadi ya raia wa Ujerumani waliokamatwa nchini humo kwa sababu za kisiasa kuwa 12. “Hii ndiyo sababu tunahitaji kuchukua hatua muhimu hapa,” alisema na kuongeza kwamba Serikali yake inapaswa kutafakari upya uhusiano wake na Uturuki. Merkel alisema Ujerumani tayari imeendeleza kwa kiasi kikubwa uhusiano wake na Uturuki, lakini hatua hii mpya ina maana huenda ni muhimu kutafakari upya zaidi. “Madai yetu kwa Uturuki yako wazi kabisa,” alisema msemaji wa Serikali ya Ujerumani, Steffen Seibert. “Tunatarajia Uturuki itawaachia huru raia wa Ujerumani ambao wamekamatwa kwa misingi isiyokuwa ya kisheria.” Mahusiano baina ya washirika hao wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO yamevurugika tangu Serikali ya Ujerumani ilipoikosoa Uturuki kuhusu ukandamizaji uliofuatia jaribio la mwaka jana la mapinduzi lililoshindwa. Mwisho | 2 |
LONDON, ENGLAND KLABU ya soka ya Manchester United ipo katika mipango ya kupata saini ya mchezaji wa kimataifa wa nchini Italia na kiungo wa timu ya Paris Saint Germain (PSG), Marc Verratti, ili kutua katika dimba la Old Trafford. Kocha mpya wa klabu hiyo, Jose Mourinho, amepanga kukitengeneza kikosi mahiri cha timu hiyo ambacho mara ya mwisho kuwa bora ilikuwa mwaka 2013 ambapo ilimaliza Ligi Kuu England ikiwa nafasi ya tano. Kwa mujibu wa mtandao wa Corriere dello lilidai kuwa United ilitenga Euro 100 ili kuipata saini ya kiungo huyo wa zamani wa timu ya Inter Milan. Kukamilika kwa usajili huo kunaweza kuvunja rekodi ya klabu hiyo ya Euro milioni 75 ya usajili wa Angel Di Maria mwaka 2014. Pia kiungo huyo kama atatua Old Trafford anaweza kuungana na mchezaji wa zamani wa PSG, Zlatan Ibrahimic ambaye yupo mbioni kutua kwenye timu hiyo. Nyota huyo ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Sweden, alitangaza hivi karibuni kuondoka klabu ya PSG. Kipindi hiki cha usajili kinaweza kuwa muhimu kwa Mourinho ambaye tayari amemaliza usajili wa Eric Bailly kutoka Villarreal huku akiwa mbioni kuipata saini ya wachezaji wawili kutoka klabu ya Juventus, Alvaro Morata na Paul Pogba. | 4 |
BERLIN, UJERUMANI RIPOTI iliyotolewa na Shirika la Waandishi wasio na Mipaka (RSF) imemtuhumu Rais wa Marekani, Donald Trump na mataifa ya Urusi na China kuwa tishio kwa uhuru wa vyombo vya habari duniani. Aidha ripoti hiyo ya mwaka 2018 imesema kushamiri kwa siasa za kizalendo barani Ulaya kumechangia kudhoofisha uhuru wa vyombo vya habari eneo hilo, ambalo awali lilikuwa salama zaidi. Kwa mujibu wa ripoti, uhasama dhidi ya waandishi na vyombo vya habari ni kitisho kikubwa kwa demokrasia duniani kote ikiwamo Ulaya. Kati ya nchi tano za juu ambako hali ya uhuru wa vyombo vya habari imeshuka zaidi, nne kati ya hizo ziko Ulaya, ambazo ni Malta, Slovakia, Jamhuri ya Czech na Serbia. Shirika hilo limeonyesha wasiwasi hasa kuhusu mauaji ya mwandishi Daphne Caruana Galizia wa Malta, yaliyofuatiwa na mauaji ya mwandishi mwingine wa habari za uchunguzi, Jan Kuciak miezi mitano baadae. Kutokana na kushamiri kwa siasa za kizalendo na viongozi ‘wababe’ Ulaya itaendelea kushuka viwango, limeonya shirika hilo. RSF imesema chuki dhidi ya wanahabari ‘si tu katika utawala wa Uturuki na Misri bali pia imeingia katika maeneo mengine. Pia ripoti hiyo imeonesha wasiwasi juu ya “udhibiti na ufuatiliaji” wa wanahabari nchini China huku Rais Xi Jinping akizidisha udhibiti wa vyombo vya habari katika maeneo ya bara la Asia. Ripoti hiyo inasema Raism huyo wa China anakaribia kuwa toleo la kisasa la utawala wa kiimla. Norway imeendelea kushikilia nafasi ya juu katika orodha ya uhuru wa vyombo vya habari kwa mwaka wa pili mfululizo huku Korea Kaskazini ikisalia katika nafasi ya mwisho kati ya nchi 180 zilizopimwa viwango hivyo. Nchi ambayo imepiga hatua kubwa katika orodha hiyo ni Gambia, ilipanda kwa nafasi 22 hadi kufikia nafasi ya 122. | 2 |
WASHINGTON, MAREKANI RAIS mteule Donald Trump huenda akamtangaza ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya mafuta ya Exxon Mobil mwenye uhusiano wa karibu na Rais wa Urusi Vladimir Putin kuwa mwanadiplomasia namba moja Marekani. Jina la Ofisa Mkuu Mtendaji huyo wa Exxon, Rex Tillerson lilijitokeza Ijumaa iliyopita kama mtu anayefaa zaidi miongoni mwa wanaopewa nafasi ya uwaziri wa mambo ya nje wa Marekani, kwa mujibu wa timu yake ya mpito. Vyanzo viwili vya habari katika timu hiyo, vimeripoti kuwa Tillerson alitarajiwa kukutana na Trump na atatangazwa kushika wadhifa huo. Awali Rais mteule alifanya mahojiano na mgombea urais wa mwaka 2012 kupitia chma chake cha Republican, Mitt Romney mara mbili ikiwamo kula naye chakua cha usiku. Lakini inasemekana sasa Trump ameachana na mpango wa kumpa wadhifa huo gavana huyo wa Massachusetts. Tillerson anapewa nafasi kubwa baada ya Meya wa zamani wa New York, Rudy Giuliani kujitoa rasmi katika orodha ya wanaofikiriwa kushika wadhifa huo. Kujitoa kwa Giuliani kumekuja baada ya uchunguzi wa kina kuhusu shughuli zake za kibiashara ng’ambo, hali ambayo timu ya Trump inaona itasababisha mgongano wa maslahi. Hata hivyo, iwapo Tillerson atateuliwa suala la mgongano wa maslahi litakuwepo kutokana na ukaribu wake na Putin pamoja na shughuli za Exxon Mobil katika nchi zaidi ya 50 katika mabara sita duniani. Mwaka 2011, Exxon Mobil ilisaini mkataba na Rosneft, kampuni kubwa ya taifa ya mafuta Urusi kwa ubia unaoshirikisha masuala ya utafiti na uzalishaji mafuta. Mwaka 2013, Rais Vladimir Putin alitoa tuzo ya juu kabisa ya urafiki kwa Tillerson, ambaye ni mpinzani mkubwa dhidi ya vikwazo vya Marekani kwa Urusi. Iwapo Trump atamteua Tillerson utaonesha dhamira ya bilionea huyo kuimarisha uhusiano wa utawala wa Putin, kama kama walivyoahidi baada ya kusifiana mara kwa mara. | 2 |
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Watimanywa alisema ingawa hakushinda, lakini anashukuru hapo alipofika.“Nawashukuru Watanzania kwa kunipigia kura na kuwa mshindi wa pili anayependwa duniani, bila wao nisingefika hapo,” alisema na kuongeza kuwa siri kubwa ya kufanya vizuri ni kujichanganya na warembo wengine duniani, hali iliyowavutia wengi na kumpigia kura.Alisema michuano hiyo imemfunza kuwa unapoenda kwenye mashindano kama hayo unatakiwa kuzungumza na kila mtu, na sio kujitenga peke yako.Watimanywa alisema mrembo aliyenyakua taji hilo la dunia kutoka Afrika Kusini alistahili kutwaa kwani hakubahatisha kwasababu alionekana tangu mapema kuwa alijiandaa.Alisema wala hasikitishwi kwa kushindwa kutwaa taji hilo kwa vile haikuwa bahati yake, na kwamba aliyestahili ni huyo wa Afrika Kusini, Rolene Strauss kutokana na sifa.Kuhusu kufungiwa kwa mashindano hayo, Watimanywa alisema kuna umuhimu mkubwa wa kufanyika kwa majadiliano kati ya Kamati ya Miss Tanzania na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa ajili ya kutafuta muafaka.Alisema mashindano hayo sio tu yalikuwa yanainufaisha Kamati, bali pia warembo wengi walikuwa wakipata ajira kupitia mashindano hayo. | 4 |
Kwa miaka mingi, Uganda imekuwa ikisubiri medali kwa mchezaji mmoja mmoja katika mashindano hayo ya dunia ya nusu marathon, ambapo sasa itabidi kuendelea kusubiri medali hiyo hadi mwaka 2020 Gdynia, Poland.Kwa mara nyingine, taifa hilo la Afrika Mashariki limeshindwa kupata nafasi ya kupanda stejini kutokana na kuendeleza ukame wa medali katika mashindano haya ya riadha, ambapo kwa mara ya mwisho ilipata medali mwaka 2004 wakati wanariadha watatu, Wilson Busienei, Martin Toroitich na Joseph Nsubuga waliposhinda medali ya shaba kwa timu mjini New Delhi, India.Jumamosi, Uganda ilitwaa kiasi hicho cha fedha baada ya kushika nafasi ya tano kwa upande wa timu katika mbio za wanaume za kilometa 21, mbio ambazo mshindi ni Mkenya, Geoffrey Kamworor aliyeshinda mbio hizo kwa mara ya tatu mfululizo.Kamworor, ambaye alichomoka kwa kasi zikiwa zimebaki kilometa nne kabla ya kumalizika kwa mbio hizo, alishinda kwa kutumia saa 1:02 na kuongeza taji la mwaka 2014 na 2016 huko Copenhagen na Cardiff.Hatahivyo, bado Fred Musobo ndiye mwanariadha bora wa Uganda baada ya kumaliza katika nafasi ya 20 baada ya kuposti muda wake bora binafsi wa saa 1:01:38. Hilo lilimfanya kocha wa Uganda, Gordon Ahimbisibwe kutamka awali kuwa Kenya walikuwa wakiihofia Uganda kabla ya kufanyika kwa mbio hizo.Chakuvutia zaidi, Jackson Kiprop ndiye mwanariadha wa mwisho wa Uganda kumaliza ndani ya 10 bora wakati alipomaliza katika nafasi ya saba katika mashindano yaliyofanyika Karvana, Bulgaria miaka sita iliyopita.Ethiopia iliiongoza Kenya na Bahrain katika orodha ya medali katika timu kwa upande wa wanaume na wanawake, ambapo Jemal Yimer, Getanneh Molla na Betesfa Getahun walikosa nafasi ya kupanda stejini lakini walimaliza katika nafasi ya nne, tano na sita.Kwa upande wa wanawake, Muethiopia Netsanet Kebede kidogo avunje rekodi ya dunia kwa sekunde 14 alipomaliza kwa kutumia saa 1:06:11, wakishinda zawadi ya dola za Marekani 50,000. | 4 |
TIMU ya KMC, jana ilichomoza na ushindi wa pointi tatu muhimu dhidi ya Biashara United baada ya kuibanjua kwa mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.Katika mchezo huo ushindi wa KMC ulipatikana kupitia mabao yaliyofungwa na wachezaji Serge Tape dakika ya 29, na la pilli likifungwa na Kenny Ally dakika ya 57 huku bao la kufutia machozi la Biashara likipatikana dakika ya 64 kupitia kwa Ramadhan Chombo.Ushindi huo ni wa pili kwa KMC baada ya kucheza mechi 10 na kujikusanyia pointi nane zinazowafanya kupanda kidogo kwenye msimamo wakitoka nafasi ya 19 hadi ya 15. Huku wapinzani wao Biashara waliokuwa wanashikilia nafasi hiyo ya 15 wakishuka nafasi moja hadi nafasi ya 16 licha ya kuwa na pointi sawa na KMC wakitofautiana kwa uwiano wa mabao.Mchezo huo ulianza kwa kasi kila timu ikicheza kwa kujilinda zaidi kuhofia kufanya makosa ambayo yangewagharibu kufungwa bao la mapema. Pamoja na hali hiyo lakini wenyeji KMC walioneka kuwa bora kadri dakika zilivyokuwa zinaendelea kwa kufanya mashambulizi. | 4 |
Mwandishi Wetu, Dar
es Salaam Rais John Magufuli
Rais amemualika, Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuzindua kongamano la kwanza
la biashara kati ya nchi hizo mbili. Kongamano hilo la
biashara kati ya Tanzania na Uganda linatarajiwa kufanyika Septemba 6-7 mwaka
huu katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini
Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda
na Biashara, Innocent Bashungwa amesema Rais Museveni ataambatana na wafanyabiashara
kutoka nchini kwake ili kukutana na wafanyabaishara wa Tanzania na kueleza kuwa
lengo la kongamano hilo ni kutangaza fursa na kuhamasisha biashara na uwekezaji
zilizoko Tanzania na Uganda. “Serikali itapata
fursa ya kuongea na wafanyabiashara hao ili kuangalia changamoto za kufanya
biashara katika nchi hizo mbili. Vile vile Serikali zetu zitashirikiana
kuzitatua, kuangalia fursa zilizopo, kuongeza biashara katika nchi hizo mbili
na kuhamasisha uwekezaji. “Sisi Tanzania
tumekuwa tukiwauzia chakula na vifaa vya viwandani, kwakuwa tunajenga uchumi wa
viwanda ni fursa kwa Watanzania kushiriki kwenye kongamano hilo ambalo litakuwa
na tija kubwa kwetu kama nchi,” amesema Bashungwa. “pamoja na
mambo mengine, Bashungwa pia amesema Rais Magufuli analeta wakuu wa nchi
mbalimbali ikiwemo Uganda ili kuwaonesha fursa tulizonazo pamoja na kujenga
mtandao mpana wa biashara. Aidha, amesema mbali
na kongamano hilo, pia kutakuwa na maonesho ya bidhaa za Tanzania ambapo
Watanzania watapata fursa ya kuonesha bidhaa za kilimo na za viwandani, taasisi
za umma na sekta binafsi zinazosaidia katika mnyororo wa thamani za biashara. “Ujio huo wa
wafanyabiashara utakuwa ni fursa ya kuunganisha wafanyabiashara wa Tanzania na
nchi hiyo kukuza wigo wa biashara, kupata masoko mapya pamoja na kutatua
changamoto na kujenga mazingira mazuri zaidi ya kufanya biashara,” amesema. Katika hatua
nyingine Bashungwa amewahamasisha wazalishaji wa bidhaa za kilimo,
wafanyabaishara na wamiliki wa viwanda kutoka mikoa yote ya nchini kujitokeza
kushiriki. Amesema mwelekeo wa
Serikali ya Tanzania ni kujenga uchumi wa viwanda hivyo ni fursa kwa Watanzania
kutumia kongamano hili kwa sababu Serikali inazidi kuweka mazingira wezeshi ya
kufanya biashara nchini, kujenga viwanda na kufuatilia masoko mbalimbali lengo
ni kutaka uuzaji wa bidhaa nchini Uganda uongezeke. | 3 |
Janeth Mushi, Namanga Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Ummy Mwalimu, amewataka wataalamu wa afya maeneo ya mipakani kote
nchini kuongeza umakini wakati wa ukaguzi kwa wasafiri wanaopita katika
maeneo yao na si kupima joto la mwili pekee. Waziri Ummy ameyasema hayo leo Jumatano Machi 18,
katika Mpaka Namanga unaotenganisha Tanzania na Kenya wakati alipokuwa akifanya
ukaguzi ukaguzi katika eneo hilo. Amesema ni muhimu kufanya ukaguzi wa kina zaidi
ikiwamo kuhoji wasafiri kabla ya kuwaruhusu kupita ili kubaini historia ya
maeneo waliyotoka. “Maofisa afya mipakani tunatakiwa tuweke umakini
zaidi katika ukaguzi wa wasafiri na watu wanaopita katika maeneo yetu siyo
kuangalia joto la mwili tu. “Jana nilikuwa naangalia China kuna mtu
amemeza vidonge vya kushusha homa kusudi aweze kupita, maofisa afya ni wajibu
wenu kufanya uchunguzi zaidi. “Kwa mfano kesi ya Isabela, wangepata muda wa
kumuuliza zaidi angeweza kusema alikwenda Ubelgiji, Sweden na wangeenda mbali
zaidi wangemuuliza una dalili zozote angesema nina kikohozi. Kwa hiyo hakuna
muda wa kulaumiana ni kuhakikisha maofisa afya wanaongeza umakini,” amesema. Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ameiomba
serikali kuongeza wataalamu wa afya na vipimo vya kisasa maeneo ya mipakani
hasa wa Namanga kutokana na idadi kubwa ya wanaopita kwa sasa wakiwamo
wanafunzi waliokuwa wanasoma nchini Kenya. | 0 |
RAIS John Magufuli ameitaja miradi 17 ambayo serikali inaitekeleza kwa maendeleo ya wananchi kutokana na kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha. Alitoa kauli hiyo jana wakati akilifungua rasmi Jengo la Tatu la Abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.Rais Magufuli alisema nidhamu katika matumizi ya fedha za serikali ndiyo iliyofanikisha utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo nchini kwa matrilioni ya fedha za wananchi. Amesema fedha hizo zimetokana na jitihada za serikali za kuwabana watendaji mafisadi waliokuwa wakiiba fedha za umma na kukwamisha juhudi za serikali za kuwaletea wananchi maendeleo.Kwa mujibu wa Rais Magufuli, miradi inayotekelezwa na serikali kwa mafanikio makubwa kwa fedha zinazotokana na kodi za wananchi ni Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa gharama ya Sh trilioni 7.5, Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa mto Rufiji katika Bonde la Mto Rufiji mkoani Pwani kwa Sh trilioni 6.5 na ujenzi wa barabara za juu makutano ya Ubungo Dar es Salaam kwa gharama ya Sh bilioni 247. Miradi mingine ni ujenzi wa daraja la Kigongo – Busisi katika Ziwa Victoria mkoani Mwanza ambalo litakuwa refu katika Afrika Mashariki na Kati kwa gharama ya Sh bilioni 696.2, ujenzi wa Daraja la Selander jijini Dar es Salaam kwa gharama ya Sh bilioni 270, ujenzi wa barabara ya kutoka Kimara Dar es Salaam hadi Kibaha Pwani ya njia nane kwa gharama ya Sh bilioni 140.“Watanzania tumeamua kujenga barabara nchi nzima zaidi ya kilomita 2,115 za lami kwa gharama ya shilingi trilioni 5.37, tunajenga na kukarabati jumla ya viwanja vya ndege 15 kwa gharama ya shilingi trilioni 1.9, tuliamua kujenga na kununua rada nne katika mikoa ya Mbeya, Dar es Salaam, Mwanza na Kilimanjaro kwa shilingi bilioni 67.3, pia tumeamua kujenga meli katika Ziwa Victoria na Ziwa Nyasa kwa gharama ya shilingi bilioni 172.3 pamoja na kupanua Bandari ya Dar es Salaam, Mtwara na Tanga kwa shilingi trilioni 1.2,” alieleza Rais Magufuli. Katika kuonesha maamuzi sahihi yanayofanywa na Watanzania katika kuamua na kutekeleza miradi ya maendeleo, miradi mingine iliyotajwa kutekelezwa na serikali ni kuifufua Kampuni ya Ndege (ATCL) kwa kununua ndege mpya nane kwa Sh trilioni 1.03 na kuagiza ndege zingine mpya tatu na kufanya ndege zote kuwa 11. Mambo mengine ambayo wananchi wameyatekeleza kupitia serikali yao ni uwezeshaji wa vijana, akina mama na walemavu ambapo mpaka sasa jumla ya Sh bilioni 54 zimetolewa kwa makundi hayo matatu; ujenzi wa miundombinu katika majiji, manispaa na halmashauri kwa gharama ya Sh trilioni 1.35.“Katika sekta ya afya kuna ujenzi wa vituo vya afya 352, zahanati 30, hospitali 67, ukarabati wa hospitali 21 za zamani kwa shilingi bilioni 321, tuliamua kununua vifaa vya hospitalini kwa gharama ya shilingi bilioni 64, katika elimu tumekarabati shule kongwe 62, ujenzi wa madarasa, maabara na nyumba za walimu kwa shilingi bilioni 308.1. “Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu tangu tuingie madarakani shilingi trilioni 1.62 na elimu bure shiingi bilioni 945.987 zimetumika mpaka sasa, pamoja na fedha nyingi katika kununua dawa, kutekeleza miradi ya maji, umeme, kilimo, uvumi, mifugo na mingine ambayo ni matokeo ya maamuzi yetu,”alieleza Magufuli. Maamuzi mengine makubwa yaliyofanywa na wananchi kupitia serikali yao ni suala la kuhamia Dodoma ili Dar es Salaam ubaki kuwa mji wa biashara. Alisema katika nia ya kulifanya Dar es Salaam jiji la biashara, jumla ya Sh bilioni 660 zimetengwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami. Rais Magufuli alisema pamoja na miradi hiyo pia jengo hilo la JNIA limejengwa kwa zaidi ya Sh bilioni 700 na litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka, lakini kwa wakati mmoja linaweza kuhudumia abiria 2,800 wanaoondoka na wanaosafiri. | 3 |
Avelyn Kitomari-Dar es Salaam ZAIDI ya Asasi za Kiraia (AZAKI) 200 kutoka maeneo yote nchini zimeshiriki kuandaa andiko la namna ya kupambana na maambukizi ya virusi vya corona lengo likiwa ni kuongeza ufanisi wa kukabiliana na janga hilo. Mratibu wa Kitaifa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa alisema wameandaa mpango huo kwa kufanya tathmini na kuainisha changamoto zilizojitokeza. “Pia tumeangalia madhara mbalimbali yaliyotokea na kuona ni kwa jinsi gani wanaweza kuwa sehemu ya kuendeleza hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kupambana na janga hili. “Katika mpango mkakati wetu maeneo ambayo AZAKI imepanga kushirikiana na Serikali ni pamoja na uhamasishaji juu ya hatua za kujikinga, utoaji wa huduma,ushauri na kusaidia pale changamoto zinapojitokeza, mikakati ya kupunguza matokeo hasi , pamoja na kuweka mpango wa pamoja baina ya Serikali na sisiI”,alisema. Aliipongeza Serikali kwa hatua wanazochukuwa kukabiliana na ugonjwa huo na kusema ipo haja ya kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Faustine Ndugulile alisema Serikali itaendelea kushirikiana na AZAKI katika kupambana na maambukizi ya corona. Alisema AZAKI pamoja na wananchi wanao, wajibu wa kushirikiana na Serikali kupambana na ugonjwa huo, ambao ni janga la dunia lililoleta athari za kiuchumi na kiafya na kusabisha vifo vingi kwa muda mfupi. Mwenyekiti Shirikisho la Vyama la Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Ummy Nderiananga aliwashukuru wataalamu wa afya kwa huduma wanayoitoa kwa wananchi waliopata maambukizi ya ugonjwa huo. | 0 |
Mbali na kutowasikiliza makocha, mwanariadha Failuna Abdi alionesha utovu mkubwa wa nidhamu timu hiyo ilipokuwa ikirejea nchini kwenye Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere mbele ya viongozi wa Riadha Tanzania (RT) pamoja na wale wa Kamati ya Olimpiki (TOC) baada ya kugoma kwenda kambini Kibaha na kutokomea kusikojulikana bila kuaga.Kwa mujibu wa taarifa ya Kocha Mkuu wa timu ya riadha iliyoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, Zakarie Barie, baadhi ya wachezaji walionesha utovu wa nidhamu kambini kwa kuwabishia makocha kwa kugomea kumaliza programu za mazoezi.Barie akizungumza kwa njia ya simu alikiri kutokea kwa vitendo hivyo vya utovu wa nidhamu na kusema kuwa ameshatoa mapendekezo kwa wahusika, ambao kama wataona inafaa watawaadhibu wahusika ili iwe fundisho kwa wengine.Sehemu ya taarifa hiyo inasema: “Tabia hiyo mbaya ya kukosa nidhamu iliendelea tulipofika Dar es Salaam Airport wakati tuliporudi kutoka Australia, wakati katibu mkuu wa TOC alipokuwa akitoa mwongozo na utaratibu wa malazi na usafiri mwanariadha Failuna Abdi alionesha dharau kubwa mbele ya Katibu Mkuu wa TOC alipokataa kufuatana na wachezaji wengine na kuondoka bila kuaga. Hiyo ni dharau na kukosa nidhamu mbele ya kocha hata kwa wachezaji wenzake. Bila shaka katibu wa RT atalishughulikia na kukomesha tabia hiyo isiendelee tena.”Mbali na Failuna, mwanariadha mwingine Agustino Sulle jina lake lilienguliwa kutoka katika orodha ya wachezaji waliokwenda Australia baada ya kushindwa kuripoti katika kambi hiyo kwa madai ya kufanya hivyo baada ya kuambiwa na kocha wake, Thomas John.John pia ndiye kocha wa Failuna na Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday jana aliliambia Habari Leo kuwa kocha huyo naye anahusika moja kwa moja kwa Sulle kukacha kambi ya taifa, hivyo naye ana adhabu yake.Gidabuday alisisitiza kuwa wachezaji hao pamoja na Sarah Ramadhani ambaye alishiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, naye anahusika kwa vitendo vya utovu wa nidhamu wakati wa kambi hiyo mjini Arusha hivi karibuni ingawa hakutajwa katika ripoti ya kocha Barie.Taarifa zingine ambazo hazitathibitishwa zilisema kuwa baadhi ya wachezaji mbali na kuwa wajeuri kwa makocha, pia walikuwa wakimdharau matroni Lwiza John, huku wengine wakigoma kulala kambini na kulala kusikojulikana.Kamati ya Ufundi ya RT ilikutana Jijini Dar es Salaam juzi na kuzungumzia matokeo ya Jumuiya ya Madola pamoja na ripoti ya kocha Barie kuhusu utovu huo wa nidhamu, ambapo mapendekezo na maamuzi yamepelekwa kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Dk Singo Yussuph kwa utekelezaji.Naye Mkurugenzi wa Michezo, ambaye alikuwa mkuu wa msafara wa timu ya Tanzania iliyoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, Dk Yussuph Singo alisema kuwa waliporudi ilikuwa wiki ya bajeti, hivyo walishindwa kukutana na kufanya tathmini.Alisema kwa sasa yuko Dodoma na anasubiri apate ripoti za michezo yote na ndio atalizungumzia hilo kwa ujumla na kujua siku watakayofanya tathmini, kwani kwa sasa hata ripoti ya RT haiajaipata. Mbali na riadha, Tanzania katika michezo hiyo ya Jumuiya ya Madola ilipeleka pia timu za ngumi, mpira wa meza pamoja na kuogelea. | 4 |
['Mkufunzi wa Man United Ole Gunnar Solskjaer anahofia kwamba hatma ya kazi yake itakuwa haijulikani iwapo timu yake itashindwa kwa mabao mengi ugenini Liverpool.(Mail)', 'Baadhi ya wachezaji wamepoteza matumaini na raia huyo wa Norway anaamini baadhi yao wamekataa kumsikiliza. (Sun)', 'Solskjaer anahitaji kitita cha £300m kutumia katika dirisha lijalo la uhamisho na kumnunua mshambuliaji kama vile mshambuliaji wa Tottenhama na England Harry Kane,26, kulingana na winga wa zamani Lee Sharpe. (Talksport)', 'Kane anafaa kuondoka Tottenham na badala yake kuhamia Manchester City, kulingana na beki wa zamani wa England Glen Johnson. (Betdaq, via Independent)', 'Liverpool huenda ikapokea kitita cha £4.5m kati ya kile cha £84m wanazodaiwa na Barcelona baada ya kumnunua kiungo Philippe Coutinho, 27, ambaye alihamia Nou Camp mwaka 2018. (Mirror)', 'Everton inafikiria kumnunua mchezaji anayelengwa na Manchester United Moussa Dembele katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari. Mshambuliaji huyo wa Ufaransa , mwenye umri wa miaka 23 anaweza kugharimu £40m kutoka Lyon. (Star)', 'Chelsea na mshambuliaji wa Marekani Christian Pulisic, 21, amekiri kukasirishwa kwake kwa kukosa muda wa kucheza zaidi tangu uhamisho wake wa £58m kutoka Borussia Dortmund. (Guardian)', 'Mshambulaji wa Arsenal Gabriel Martinelli, 18, anakabiliwa na chaguo katika hatma yake ya kimataifa kwa kuwa anahitajika na Itali pamoja na Brazil. Alizaliwa nchini Brazil lakini lakini babake ni raia wa Itali hivyobasi anaweza kuwakilisha timu zote mbili.. (Mirror)', 'Mshambuliaji wa Venezuela Salomon Rondon, 30, amekiri kwamba angependelea kuandikisha mkataba wa kudumu na klabu ya Newcastle lakini akasema kwamba hakupatiwa fursa kubadili uhamisho wake wa mkopo wa msimu uliopita kuwa kandarasi ya kudumu na hivyobasi akaelekea katika klabu ya China ya Dalian Yifang. (Newcastle Chronicle)', 'Mkufunzi Roy Hodgson anasema kwamba klabu ya Crystal Palace italazimika kumsaini mshambuliaji mpya mwezi januari iwapo wanataka kumaliza katika orodha ya timu sita za kwanza katika jedwali na pia analenga kuwasajili mabeki wawili wapya wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. (Standard)'] | 4 |
SERIKALI imetakiwa kuleta mabadiliko ya sheria yatakayoiwezesha Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kuwa mamlaka ili isimamie sekta hiyo ipasavyo. Wabunge waliitaka serikali kuleta mabadiliko hayo wakati wakichangakia jana katika mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii.Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF) alisema iwapo TFS itapandishwa hadhi itaweza kusimamia ipasavyo ukuaji na uendelezaji wa sekta ya misitu nchini. “Ikiwa mamlaka, TFS itakuwa na madaraka yake na pia kupanga maendeleo ya sekta kama zilivyofanya Tanapa, Ngorongoro na mamlaka zingine, wakati umefika wa kufanya mabadiliko,” alisema Sakaya.Mbunge wa Viti Maalumu, Dk Immaculate Semesi (Chadema), ameitaka TFS kuhangalia jinsi ya kulinda na kutunza misitu hasa ile iliyopo kwenye ukanda wa bahari ili kujilinda na majanga na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi. “Tumekata miti katika ukanda wa Bahari ambayo ni kinga kwetu wakati wa majanga, tushukuru kimbuga Kenneth hakijatufikia, kama ilivyotabiriwa la sivyo madhara yangekuwa makubwa sana,” alisema Dk Semesi.Mbunge wa Viti Maalumu, Susan Kiwale (Chadema) akichangia hotuba hiyo alisema umefika wakati sasa wa serikali kuibadilisha TFS kuwa mamlaka kama ilivyo Tanapa ili ifanye kazi zake kwa ufanisi zaidi.Katika hatua nyingine, Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania imepewa jukumu la kuanzisha majaribio ya upandaji miti, ukuaji, uhifadhi, matumizi ya miti ya asili na kigeni, kuratibu tafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu matumizi ya teknolojia bora, mpya ya miti, hifadhi ya udongo, wanyama na mimea.Hayo yalielezwa juzi na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla wakati akitoa hotuba yake wakati wa kuwasilisha bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020. Alisema taasisi hiyo imeanzisha majaribio 30 ya utafiti wa upandaji sahihi wa miti kwenye eneo la hekta 95 katika Kanda ya Ziwa, Kati, Mashariki, Kaskazini na Nyanda za Juu Kusini.Kwa mujibu wa Waziri Kigwangalla, matokeo ya majaribio hayo yataongeza wigo wa spishi za miti ya asili zitakazokuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.Alisema taasisi imekusanya na kusambaza taarifa kuhusu janga la moto wa misitu kwa kutumia takwimu za satelaiti na kuwa taarifa hiyo inaonesha kuwa janga la moto ni kubwa na limeathiri eneo la misitiu lenye kilometa za mraba 100,903 ambao ni sawa na asilimia 11 ya eneo lote la Tanzania Bara.Aliyataja maeneo yaliyoathirika kuwa ni mikoa ya Lindi, Katavi, Mbeya, Tabora na Ruvuma na kuongeza kuwa wizara kwa kushirikliana na wadau inaendelea kuelimisha umma kuhusu kuchukua tahadhari na kuzuia moto wa misitu.Katika kupunguza madhara ya moto kwenye mashamba ya miti na misitu ya hifadhi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umefanya kampeni za uhamasishaji wa matumizi sahihi ya moto katika vijiji 318 vilivyoko karibu na amshamba ya miti na misitu ya asili. | 3 |
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM FAINALI ya Michuano ya Kombe la Azam, inatarajia kufanyika leo kwa timu ya Azam kukabiliana na Lipuli FC, katika mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi. Azam FC waliingia hatua ya fainali baada ya kuifunga KMC bao 1-0 kwenye mchezo wa nusu fainali uliopigwa Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam. Wakati wapinzani wao Lipuli FC waliingia hatua hiyo baada ya kuifunga Yanga mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Samora, Dar es Salaam. Mchezo huo utakuwa na ushindani mkubwa kutokana na Azam FC kuhitaji ubingwa ili wapate fursa ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani baada ya kukaa kwa muda mrefu bila ya kupata nafasi hiyo. Timu hiyo itashuka dimbani ikiwa na morali ya juu baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 kwenye mchezo wao wa mwisho wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Yanga katika Uwanja wa Taifa jijini hapa. Wanalambalamba hao wataivaa Lipuli wakiwa na nguvu zaidi kutokana na baadhi ya wachezaji wao waliokuwa majeruhi hali zao kuimarika. Upande wao Lipuli watakuwa wakihitaji kuandika historia kwa mara ya kwanza ya kutaka kutwaa ubingwa huo ili wapate fursa ya kushiriki michuano ya kimataifa. Timu hiyo ambayo ilipanda daraja katika msimu wa mwaka 2017/18, imekuwa ikionyesha ushindani mkubwa hasa katika timu kongwe imepania kuendeleza ubabe kama walivyofanya katika mchezo wao dhidi ya Yanga. Tayari Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limemtangaza Hance Mabena, kutoka Tanga kuwa mwamuzi wa mchezo huo. Katika mchezo huo watatumika waamuzi sita kwa mara ya kwanza kwenye historia ya soka Tanzania ambapo Mabena atasaidiwa na jumla ya waamuzi watano (wawili wa pembeni, wawili kwenye magoli na mwamuzi mmoja wa akiba). Taarifa ya TFF iliyotolewa jana, Mabena, atasaidiwa na Mohamed Mkono kutoka Tanga kama mwamuzi msaidizi namba moja, Ferdinand Chacha kutoka Mwanza kama mwamuzi msaidizi namba 2, Abubakar Mturo kutoka Mtwara atakuwa ni mwamuzi wa akiba. Akizungumzia mchezo huo kocha mkuu wa Azam FC, Abdul Mingange, alisema anawaheshimu Lipuli FC kwani hawakufika hapo kwa kubahatisha hivyo lazima wawe makini. “Tumejiandaa vya kutosha kuhakikisha tunapata ushindi kwenye mchezo huu, ukizingatia ni muda mrefu timu yetu haijashiriki michuano ya kimataifa,” alisema. Kocha msaidizi wa Lipuli FC, Selemani Matola, alisema licha ya Azam FC kuwa ni timu nzuri hiyo haiwatishi kwani waliingia hatua hiyo kwa kuifunga klabu kubwa. “Tumefanya maandalizi mazuri hivyo tutatumia udhaifu wa wapinzani wetu Azam FC kuhakikisha tunapata ubingwa na kutwaa kombe hili na kuandika historia kwenye timu yetu,” alisema. | 4 |
RAIS John Magufuli ameinyooshea kidole Wizara ya Maji na wakandarasi wa maji akisema inatumia mabilioni ya fedha kutekeleza miradi ya maji ambayo mingi haina matokeo mazuri, isiyokamilika na mingine imekuwa hewa.Aidha, amesema serikali ya sasa haina mpango wa kuongeza mkoa mwingine kiutawala kwa sababu hata iliyopo bado ni mingi na inatumia fedha nyingi, hivyo ni bora fedha hizo zikaongezwa kwenye huduma za jamii kama ujenzi wa vituo vya afya, shule na ujenzi wa barabara huduma zinazowafaidisha wananchi wengi.Rais Magufuli alisema hayo jana wilayani Tunduru ikiwa ni siku yake ya pili ya ziara ya siku sita katika Mkoa wa Ruvuma baada ya kumaliza ziara ya siku tatu mkoani Mtwara. Akizungumzia kabla ya kufungua barabara ya Namtumbo – Kilimasera – Matemanga – Tunduru yenye urefu wa kilometa 193 iliyojengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 100, Rais Magufuli alisema Wizara ya Maji inaongoza kwa kuwa na wakandarasi wa ovyo ambao hawatumii elimu zao vizuri kwenye matendo katika kutatua changamoto ya maji nchini.Alisema wakandarasi wa wizara hiyo wanaongoza kwa kuwa wakandarasi wa ovyo nchini ambao hawatumii elimu yao kuiweka kwenye vitendo kwani nchi ina vyanzo vingi vya maji ila maeneo mengi hayana huduma hiyo na miradi inayotekeleza mingi haikamiliki.“Wewe Waziri (akimgeukia Profesa Makame Mbarawa), nilidhani nimekupeleka huko (Wizara ya Maji) ukawabadilishe hawa wahandisi wa maji, lakini naona hata hujafanya, kama kuna wizara ina wahandisi wa ovyo ni wa maji, mjipange. Mnatumia mabilioni ya fedha kwenye miradi mingi na haina matokeo mazuri,” alisema Rais Magufuli. Aidha, aliwataka wakandarasi wa maji kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanakamilisha miradi hiyo kwa wakati ili kuondoa kero kwa wananchi.“Lazima tuwe na mabadiliko mapana, hapa Tunduru, barabara yote hii hadi Namtumbo hadi Songea, ukiambiwa nchi haina maji hata watu wa mataifa kama Ulaya na kwingineko wanatucheka sana, wanatuona ni watu wasiojua kufikiri hasa kwa sisi viongozi na watendaji wa maji,” alisema Rais Magufuli. Aliwashauri kuwa kila mwenye maeneo ya mito ambayo madaraja yamejengwa na yanapitisha maji wachimbe mabwawa makubwa na wafunge mota kusambaza maji hayo kwenye maeneo yenye uhitaji.Alisema nchi ina Mto Ruvuma ambao haukauki mwaka mzima, lakini wakazi wa maeneo hayo hawana maji na kusema hilo ni jambo la aibu na uzembe wa hali ya juu. Akizungumzia ombi ya Wilaya ya Tunduru kufanywa mkoa, Rais Magufuli alisema katika utawala wake haoni sababu ya kuwa na mikoa mingi kama iliyopo na badala yake mikoa hiyo ingeweza kuunganishwa ili kupunguza gharama za uendeshaji wake na fedha hizo kupelekwa kuboresha huduma za jamii.“Siwezi ongeza mkoa mwingine, ombi lenu la eneo hili kuwa mkoa hapana, siwezi toa fedha kujenga Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, bali fedha nitatoa shilingi milioni 200 muongezee mjenge hospitali hii itakayohudumia wananchi wengi,” alisisitiza Rais Magufuli, huku akimuagiza Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo kuwapa fedha hizo wana-Tunduru.Alisema idadi ya mikoa iliyopo hivi sasa nchini haikuwa na sababu kwa kuwa ofisi nyingi za wakuu wa mikoa zinatumia fedha nyingi kiutawala ambazo haziwanufaishi moja kwa moja wananchi wa kawaida. “Sitoi fedha kujenga ofisi ya RC, kwanza ukienda kumuona kuna urasimu mrefu, utaambiwa una miadi naye, wewe ni nani umetokea wapi, na utaishia kutomwona, si bora fedha hizo zikajenge shule, vituo vya afya na barabara ambazo watapita wananchi na kuwasaidia kuinua uchumi wao,” alisema Rais Magufuli.Awali akizungumzia hali ya maji mkoani Ruvuma, Waziri Maji, Profesa Mbarawa alisema mkoa huo unazalisha lita za maji milioni 1.6 na zinasambazwa kwa wakazi 250,000 ambao ni sawa na asilimia 62 ya wananchi wote. Alisema changamoto kubwa ya maji mkoani humo ni miundombinu ya maji huku akitoa mikakati ya wizara kuwa imepanga kutekeleza aina mbili za miradi ili kupunguza kero za maji.Profesa Mbarawa alisema miradi hiyo miwili, moja ni wa muda mfupi ambao jana wametangaza zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya Sh milioni 300, na ndani ya miezi mitatu mkandarasi atakayepatikana akamilishe ujenzi huo. Kwenye mradi wa pili ni wa muda mrefu ambao wizara inaendelea na ujenzi wa miundombinu ya maji ya gharama ya Sh bilioni 16.2 katika maeneo tofauti yakiwemo Matemanga, Mpina, Mbesa na Nandembo.Katika eneo la Nandembo, mradi umekamilika ila kisima hicho kirefu kimekauka maji. Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa alisema Sh bilioni 88 zimetumika kuwalipa wakandarasi wa maji nchi nzima na hivyo hakuna mkandarasi aliye kwenye eneo la mradi anayedai malipo.Kutokana na kauli hiyo, Rais Magufuli aliwataka wakandarasi hao kufanya kazi kwa bidii na kuacha visingizio huku akiitaka wizara kuwa wakali na wakandarasi watakaokwamisha utekelezaji wa miradi kwa kuwa wameshalipwa. “Kuweni wakali na hawa wakandarasi, hatuwezi kuendelea kufanya kazi kwa kubembelezana, lazima muwe wakali miradi ikamilike,” alisisitiza Rais Magufuli. | 3 |
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40) na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu. | 5 |
MWILI wa mwanafunzi Sperius Eradius aliyekufa Agosti 27, mwaka huu baada ya kupigwa viboko na Mwalimu Respicius Mtazangira Shule ya Msingi Kibeta Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, umezikwa Kijiji cha Kitoko Kata ya Mabunda wilayani Muleba, nyumbani kwa baba mzazi, Eradius Petro.Katika maziko hayo, serikali iliwakilishwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Joseph Kandege, ambaye katika salamu za serikali, aliihakikishia familia, ndugu, jamaa na wananchi waliojumuika kumuaga Sperius itasimamia haki hadi ipatikane kwa waliohusika na mauaji.“Sisi tunawaacha watoto wetu waende shule kama sehemu salama tukiamini ndiyo sehemu salama na ya kujifunzia na siyo chuo cha mafunzo ya viboko. Jambo hili haliwezi kuachwa likapita hivi hivi. Tuseme inatosha na iwe fundisho kwa wengine,” amesisitiza Kandege aliyetoa ubani wa serikali Sh milioni mbili.Aidha, aliiomba familia ya marehemu kuwa na subira kwa wakati huu mgumu wa kupoteza mpendwa wao huku akisema msiba huo sio wao tu, bali ni msiba wa taifa zima.Aliishukuru Serikali ya Mkoa ilivyoshughulikia tukio hilo tangu lilipotokea Agosti 27, mwaka huu hadi hatua ya kuupumzisha mwili wa mwanafuzi huyo wa darasa la tano aliyefariki kutokana na kipigo cha mwalimu huyo wa nidhamu kwa madai ya kuiba mkoba wa mwalimu wake wa kike alipoenda kumpokea.Baba mlezi, Mchungaji Justus Balilemwa amesema Sperius alizaliwa Mei 2005 na baada ya kuzaliwa mama yake aliaga dunia, hivyo kuchukuliwa na kupelekwa Ntoma kituo cha kulelea watoto yatima na baada ya mwaka mmoja alimchukua na kuishi na kumlea kama mtoto wake hadi mauti yalipomkuta.“Kinachonisikitisha leo hii ni kuwa tulimchukua Sperius Eradius akiwa mzima, lakini leo tumerudisha sanduku, haikuwa nia yetu tulitamani mtoto huyu atimize ndoto zake kwani alikuwa mchangamfu na alimjua Mungu kwa kuimba na kumtukuza Mungu katika kwaya, mfano kwaya ya Kagoma,” alieleza.Baba yake mzazi, Eradius Petro akitoa neno kwa wananchi waliofika kumfariji katika maziko hayo, alisema anamwachia Mungu kwa yaliyotokea, bali anaishukuru serikali kwa kulifuatilia tukio hilo kwa karibu.Pia alitoa ushirikiano nyumbani kwa baba mlezi tangu tukio linatokea hadi kwenye maziko. Uongozi wa Mkoa wa Kagera tangu kutokea kwa mauaji hayo, uligharamia mahitaji yote katika familia ya baba mlezi na kugharamia jeneza la kumhifadhia marehemu pamoja na usafiri wa kusafirisha mwili wa marehemu, familia, ndugu na jamaa wa Sperius kutoka Kibeta kwenda Kitoko kwa ajili ya maziko hayo. | 3 |
Ramadhani Hassan WIZARA ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesema Serikali imekuwa ikichukua hatua bila kupendelea chombo chochote cha habari kinachobainika kukiuka sheria na taratibu ikiwamo kutoa habari za uongo. Hayo yalielezwa
bungeni jana na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Juliana Shonza wakati akijibu
swali la nyongeza ya Mbunge wa Konde, Khatib Said Haji (CUF). Katika swali
lake, mbunge huyo alidai kuwa ameshuhudia baadhi ya vyombo vya habari,
hususani magazeti yakipewa adhabu ya kufungiwa kwa kutoa habari za uongo,
lakini kuna mengine ambayo hayachukuliwi hatua zozote pamoja na kwamba
yanadhalilisha na kuchafua watu. Alihoji ni
kwanini Serikali haichukui hatua kwa vyombo hivyo pamoja na wamiliki wake. Akijibu swali
hilo, Shonza alisema suala hilo halina ukweli kwa kuwa Serikali inafanya kazi
kwa kusimamia sheria na kanuni zilizopo. “Mara zote
ndani ya Bunge tumekuwa tukifafanua kwamba wizara tumekuwa tukichukua hatua kwa
magazeti yanayokiuka sheria. “Si kweli kwamba
hatuchukui hatua kwa magazeti ya Tanzanite kama alivyosema mbunge, tumeshajibu
mara kadhaa humu ndani kwamba tumeshawaandikia onyo pamoja na mengine
yaliyokuwa yanakiuka sheria,” alisema Shonza. Alisema kuwa
sheria ya habari inaeleza kwamba kabla ya kuchukua hatua yoyote kwa chombo
chochote cha habari, cha kwanza wanapaswa kupewa onyo mara ya kwanza. “Tunatoa
nafasi kwa mara ya pili, pale ambapo tunaona kwamba hali hiyo inazidi ndio
tunachukua hatua,” alieleza Shonza. Alisema hatua
hizo zimekuwa zikichukuliwa bila upendeleo. “Sisi kama
wizara tumekuwa tukichukua hatua pale ambapo tunaona tumeshaonya mara kadhaa,
lakini bado hawajajirekebisha,” alisema Shonza. Katika swali la
msingi, mbunge huyo alisema ni kosa la jinai kwa mtu au vyombo vya habari
kutoa, kuandika, kusambaza au kutangaza habari za uongo. Alihoji Jeshi
la Polisi linachukua hatua gani stahiki kwa watu au vyombo vya habari
vinavyofanya makosa hayo. Akijibu swali
hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alisema jeshi hilo
linao utaratibu unaotumika pindi mtu anapokuwa ametenda makosa ya jinai ambapo
ushahidi hukusanywa kisha jalada huandaliwa kwenda kwa Mwanasheria wa Serikali
na ushahidi ukijitosheleza mtuhumiwa hufikishwa mahakamani. Alisema kuwa Serikali
ina mamlaka kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari Na. 12 ya mwaka 2016,
ambapo inaelekeza kuchukua hatua kwa chombo cha habari kilichotoa taarifa za
uongo, ikiwa ni pamoja na kufuta leseni au kusimamisha leseni kwa muda pale
ambapo chombo cha habari kimekiuka masharti ya leseni hiyo. | 3 |
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi. Kwa misingi kama hiyo sisi kama chombo cha habari tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk. Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia. Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”. Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi, Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii. Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo. Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge. viongozi wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo. | 5 |
Na AVELINE KITOMARY-MOROGORO KATIKA kuhakikisha udhibiti wa vifaa bandia sokoni unafanikiwa, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imesema kwa mwaka wa fedha 2019/2020 iliondoa sokoni paketi 17,076 za kondomu kwa kushindwa kukidhi vigezo vinavyotakiwa. Hayo yalisemwa jana mkoani Morogoro na Kaimu Mkurugenzi wa Dawa na Vifaa Tiba, Akida Khea wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari katika kikao kazi cha uhamasishaji wa waandishi wa habari kuhusu usimamizi wa Sheria ya Dawa na Vifaa Tiba sura 219. Khea alisema bidhaa hizo zilizoondolewa ni zile feki ambazo hazikidhi matakwa ya viwango, zinazoweza kuwa na madhara na nyingine ni zile ambazo zilikuwa zikiuzwa kwa kutumia jina la mtu mwingine. “Kwanza kabla ya kondomu kuingia sokoni huwa tunapima ubora wake, kama kiwango cha mafuta, ustahimili wa matumizi na urefu wake, hivyo endapo tukipima na tukakuta haina vigezo tunaizuia kuingia sokoni. “Pia licha ya hiyo, huwa tunafanya ukaguzi katika maduka mbalimbali hapa nchini kwa kuangalia ubora wa bidhaa zilizopo na kama muda wa matumizi ya bidhaa hizo hazijaisha, hivyo tuko makini katika udhibiti wa usalama wa ubora wa bidhaa,” alieleza Khea. Alisema kondomu zilizoondolewa sokoni ni takribani aina tano ambazo ni Life Guard, Ultimate, Maximum Classic, Prudence na Chishango. Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa TMDA, Adam Fimbo, alisema mamlaka hiyo inafanya kazi za udhibiti ili kuhakikisha afya ya wananchi inakuwa salama. “TMDA inafanya ukaguzi mara kwa mara ili kuhakikisha hamna bidhaa bandia sokoni na kama zikipatikana hatua za kisheria zinachukuliwa kwa watu wanaokiuka taratibu zilizowekwa,” alifafanua Fimbo. Alisema katika kipindi cha miaka mitano, Serikali imejenga viwanda 16 kwa ajili ya dawa na vifaa tiba ili kuhakikisha vinapatikana nchini. “Tumepunguza masharti ili kuruhusu viwanda kujengwa, hiki ni kitu kikubwa kwani Serikali inaendelea kuhamasisha uchumi wa viwanda, hili ni jambo kubwa kwetu,” alisema Fimbo. | 3 |
Na ELIUD NGONDO, MBEYA
WATU wanne, wamefariki dunia na wengine wamejeruhiwa baada ya kufukiwa kwenye shimo walipokuwa wakichimba dhahabu.
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, aliwaambia waandishi wa habari jana, kwamba tukio lilitokea eneo la Nanyuki, Kijiji cha Itumbi, Kata ya Matundasi, Wilaya ya Chunya, mkoani Mbeya.
Katika maelezo yake, Kamanda Kidavashari, alisema tukio hilo lilitokea jana asubuhi na kwamba wakati wa tukio hilo, kulikuwa na wananchi zaidi ya 50 waliokuwa wamevamia shimo hilo la dhahabu linalomilikiwa na Vincent Minja, mkazi wa Dar es Salaam.
“Inasemekana watu walikuwa wamejazana kwenye shimo hilo baada ya kupata taarifa kuwa linatoa dhahabu nyingi.
“Kwa hiyo, walikuwa wanachimba bila tahadhari na kusababisha shimo kuporomoka na kuwafukia watu 11,” alisema Kamanda Kidavashari.
“Lakini, watu wale tunawachukulia kama wezi kwa sababu walivamia eneo lenye leseni ya mtu mwingine,” alisema.
Aliwataja waliofariki kuwa ni Andrew Paulo (26), Mark Fredrick (22) na Isack Mwanjale (30) wote wakazi wa Kijiji cha Itumbi na Hamis Mailosi (25) mkazi wa Kijiji cha Mapogoro.
Kwa upande wa waliojeruhiwa, aliwataja kuwa ni Saimon Majaliwa (25), mkazi wa Itumbi, Mazoea Mahona (25), mkazi wa Mkoa wa Tabora, Ben Bahati (23), mkazi wa Kijiji cha Mapogoro na James Alinanuswe (26), mkazi wa Tukuyu, wilayani Rungwe.
Diwani wa Kata ya Matundasi, Kimo Choga, alisema wananchi hao walianza kuvamia eneo hilo Jumatatu wiki iliyopita na kwamba walizuiliwa na mwenye leseni ya eneo hilo lakini hawakumwelewa.
“Ilipofika Alhamisi, wananchi hao walielimishwa vizuri na kukubali kusimamisha kazi ya kuchimba madini hayo baada ya mwenye eneo kuwaeleza kuwa kufikia Jumatatu (jana), atakuwa ameweka utaratibu mzuri wa namna ya kuchimba.
“Lakini, jana asubuhi walivamia tena shimo moja wakidai mmiliki wa leseni ya eneo hilo alikuwa akiendelea kuchimba, hivyo nao wakasema lazima wachimbe,” alisema Diwani Choga. | 3 |
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amesisitiza kuchukua hatua kwa watendaji wa vijiji wanaopinga kuchangia masuala ya maendeleo badala yake kutengeneza migogoro ya ardhi.Aidha, ameagiza Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru kuhakikisha wanatoa vitabu kwa watendaji wa kata ili waandike majina ya wananchi wanachangia michango ya maendeleo, ikiwemo masuala ya elimu. Gambo aliyasema hayo jana kwenye Kata ya King’ori baada ya kuchukizwa na kitendo cha baadhi ya wenyeviti wa vijiji vinane vya kata hiyo, kutengeneza migogoro pale panapohitajika kuchangia masuala ya maendeleo. Alikuwa akikagua ujenzi wa madarasa mpya ili kuhakikisha hakuna mwanafunzi ambaye atabaki nyumbani mwezi huu kutokana na uhaba wa madarasa.Alisema amechukizwa na tabia ya baadhi ya wenyeviti wa vijiji, kutengeneza migogoro ya ardhi ili kuwapotosha wananchi wasichangie maendeleo, ikiwemo ujenzi wa shule kwa kila kata. “Nitachukua hatua kwa wale wote wanaokwamisha maendeleo kwa wananchi hususan nyie viongozi wa vijiji ambao badala ya kuhamasisha ujenzi wa madarasa nyie mnaingiza migogoro ya ardhi mambo ambayo hayafanani kabisa na naomba majina ya viongozi wanaokwamisha maendeleo ili hatia zichukuliwe,” alisema Gambo.Awali Mtendaji wa Kijiji cha Nkoansiyo, Kata ya King’ori, Jackline Kimaro alisema kata hiyo ina vijiji nane huku kila kijiji kikitakiwa kutoa Sh 2,187,500, lakini vijiji vitatu vya Nsengoni, Mboreny na Mvungano havijawahi kutoa fedha za maendeleo. Awali wakijitetea wenyeviti wa vijiji, Enock Mbise kutoka Kijiji cha Mboreny na Ruben Nassari wa Nsengoni, walikiri kutohamasisha wananchi kuchangia miradi ya maendeleo kutokana na migogoro ya ardhi. Waliomba msamaha kwa Gambo kuwa watahamasisha wananchi kuchangia maendeleo na si migogoro.“Ni kweli kuna migogoro ya mipaka ya ardhi ambayo sisi wenyewe tumeikuta na kweli hatujahamasisha wananchi wachangie maendeleo kwa sababu ya migogoro hiyo tunaomba kuanzia sasa tutahamasisha wananchi wachangie maendeleo,” alisema Mbise. Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro alikiri wilaya hiyo kuwa na changamoto hiyo kwa baadhi ya watendaji vijiji kuingiza migogoro ya ardhi ili kuzuia wananchi kufanya shughuli za maendeleo.Aliagiza kupewa orodha ya majina ya viongozi hao, wanaotengeza migogoro pale wanapohitajika kuchangia masuala ya maendeleo. Aliahidi kugawa vitabu vya risiti kwa watendaji wa kata ili waandike majina ya wananchi wanachangia maendeleo. Gambo alitembelea shule za sekondari za Makiba, Maruvangu na Umoja. | 3 |
WASHINGTON, MAREKANI Serikali ya Marekani imetishia kuiwekea vikwazo Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), ikiwa itaendelea na mikakati yake ya kuwashtaki raia wake. Mahakama hiyo kwa sasa inatathmini kuwafungulia mashtaka wanajeshi wa Marekani kwa madai ya kuwatesa wafungwa nchini Afghanistan. Mshauri wa masuala ya usalama ya taifa, John Bolton, amesema mahakama hiyo si halali na kuapa kuwa Marekani itafanya kila iwezalo kuwalinda raia wake. Marekani ni kati ya nchi kadhaa ambazo hazijajiunga na ICC ilihali imekuwa mstari wa mbele kushinikiza viongozi fulani wa mataifa mengine hasa Afrika kushtakiwa. Novemba mwaka jana, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC, Fatou Bensouda alisema kuna sababu za msingi za kuamini kwamba uhalifu dhidi ya ubinadamu ulifanyika katika vita nchini Afghanistan, tangu uvamizi ulioongozwa na Marekani mwaka 2001. Bensouda alisema uchunguzi makini wa awali umemfanya aamini kwamba vigezo vyote vya kisheria vipo kuwezesha kuanza kwa uchunguzi. Lakini Bolton ameonya iwapo waendesha mashtaka wa ICC watajaribu kuanzisha uchunguzi huo, Marekani italipiza kisasi kwa kuwalenga majaji na waendesha mashtaka wa mahakama hiyo. Hiyo ni pamoja na kuwapiga marufuku kukanyaga ardhi ya Marekani na kutumia mfumo wake wa fedha. Mshauri huyo wa Rais Donald Trump alitishia pia kuwafikisha katika mahakama za nchi yake watendaji hao wa ICC. Vile vile alisema nchi yake itaziwekea vikwazo kampuni zitakazoshirikiana na mahakama hiyo yenye nchi wanachama zaidi ya 120. Tisho hilo linakuja huku mwaka uliopita ukishuhudia nchi tatu za Afrika; Burundi, Gambia na Afrika Kusini zikionyesha nia ya kujitoa kutoka mahakama hiyo na kulikuwa na hofu kuwa nchi zaidi zingefuata. Oktoba mwaka juzi, Burundi na Afrika Kusini zilimwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuelezea uamuzi wao wa kuondoka ICC. Taifa jingine la Gambia lililopo magharibi mwa Afrika lilitangaza kuwa lingejitoa kabla ya kufuta uamuzi huo baada ya kuingia madarakani Serikali mpya. | 2 |
RAIS wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Antony Mtaka (pichani) amewataka wanariadha kujitambua ili waweze kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.Hayo yalisemwa juzi jijini Dar es Salaam na Mtaka alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu sababu za Simbu kutofanya vizuri katika mashindano ya mwaka huu ya dunia ya riadha yaliyofanyika Doha, Qatar kuanzia Septemba 27 hadi Oktoba 6. Alisema kuwa Simbu ameshindwa kujitambua na ndio maana aliungana na wengine kukataa kambi ya Erdolet iliyoandaliwa na RT ili kuwawezesha wanariadha hao kupata changamoto kutoka kwa wanariadha nyota wa dunia.Wanariadha Failuna Abdi, Augustino Sulle na Stephano Huche pamoja na Simbu walikataa kambi nchini Kenya kwa ajili ya maandalizi ya mashindano hayo ya dunia. Ukimuondoa Simbu, wanariadha whao wengine walishindwa kumaliza marathon kutokana na joto kali la Doha. Mtaka alisema kuwa riadha ni mchezo binafsi tofauti na soka, ambao ni mchezo wa timu na inabidi kushirikiana na wengine ili kupata ushindi, lakini tofauti na riadha, ambapo juhudi zake ndizo zitakupa ushindi.Alisema wanariadha lazima uwe na nidhamu ili kufikia malengo, ambapo unatakiwa kujua unatakiwa kufanya nini ili kufikia malengo yako. Aliwashangaa wanariadha ambao hawana programu za maana na badala yake wamekuwa kila kukicha wakikimbia mbio mbalimbali ndogo, ambazo haziwapatii fedha nyingi badala ya kuchagua mbio chache zenye fedha nyingi.Simbu alisema kwa njia ya simu juzi kuwa anajitambua na anajua anachokifanya na siku moja atafanya vizuri zaidi katika mchezo huo, tofauti na wengi wanavyofikiria kuwa hana jipya. | 4 |
SIMBA jana iliaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kukubali kipigo cha mabao 4-1 dhidi ya TP Mazembe ya Congo DR.Wawakilishi hao wa Tanzania, walihitaji ushindi au sare yoyote ya mabao kusonga mbele baada ya kutoka suluhu nyumbani dhidi ya mabingwa hao wa zamani wa Afrika, lakini hali ilikuwa tofauti.Mchezo huo wa robo fainali ulichezwa jana kwenye uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi na kwa ushindi huyo Mazembe imetinga nusu fainali za michuano hiyo. Mabao yalifungwa na Emmanuel Okwi kwa upande wa Simba na Mazembe ni Kabaso Chongo, Meshack Elia, Tresor Mputu na Jackon Muleka.Simba ndio walitangulia kupata bao la uongozi dakika ya pili, likifungwa na Okwi baada ya kupata pasi ya kiungo Haruna Niyonzima. Mazembe walicharuka na kuanza kushambulia lango la wekundu hao na kusawazisha dakika ya 23 kupitia kwa Elia na baadaye dakika ya 38 Chongo akifunga la pili.Mbali ya kuongoza, Mazembe pia ilitawala mchezo huo tangu walipoapata bao la kusawazisha mpaka mwisho wa mchezo.Simba ilikianza kipindi cha pili kwa mabadiliko kwa kuwatoa Mzamiru Yassin na Juuko Murshid, Okwi na nafasi zao kuchukuliwa na Cletous Chama, Meddie Kagere na Rashid Juma.Mabadiliko hayo hayakusaidia zaidi ya Mazembe kuongeza kasi ya kushambulia na kuongeza bao la tatu na la nne dakika ya 62 na 73 yakifungwa na Mputu na Muleka.Mazembe walitengeneza nafasi nyingi za kufunga kama wangetulia walikuwa na uwezo wa kufunga mabao zaidi ya hayo.Lakini pia, kwa upande wa Simba dakika za mwishoni walijaribu kushambulia na kutengeneza nafasi ila hazikuzaa matunda. Simba sasa inarudi nchini kuelekeza nguvu zake kwenye kutetea taji la Ligi Kuu ambapo ina viporo tisa | 4 |
Alisema mradi huo wa nyumba unajengwa katika eneo la Iyumbu, karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma. Alisema hatua hiyo itapunguza uhaba wa nyumba za makazi na biashara katika manispaa ya Dodoma, kwa kuwa miradi mingine ya nyumba za biashara itajengwa katika eneo Meledeli.Akifafanua, Gambalagi alisema NHC itatekeleza miradi miwili ya nyumba za gharama nafuu katika Halmashauri za Chamwino na Bahi ambapo zaidi ya nyumba 50 za kuuza zitajengwa katika mwaka huu wa fedha.Alisema katika kutekeleza miradi hiyo NHC itajenga nyumba za kuuza kwa zile halmashauri zitakazoonesha zina mahitaji na utayari wa kulipia au kuwepo kwa soko la nyumba zitakazojengwa.Gambalagi alisema kwa nyumba za kupangisha, shirika linaendelea kuzifanyia matengenezo makubwa nyumba zake inazomiliki katika Manispaa ya Dodoma. Alisema hivi karibuni, shirika lilibadilisha madirisha ya kizamani na kuweka madirisha ya kisasa kwenye nyumba zake zilizopo eneo Mpwapwa ya zamani na zile zilizoko barabara ya Iringa.Alisema shirika pia limesaidia vijana kwa kila halmashauri ya wilaya, mkoani hapa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana ili kuwapa ajira na kuwaondolea umasikini. | 5 |
UFARANSA imefungua milango kwa Watanzania zaidi kusoma nchini kwao kwa serikali yake kuongeza nafasi za ufadhili kutoka 30 kwa mwaka mpaka 50.Aidha, serikali imetaka Ufaransa kuanza kufundisha lugha ya Kiswahili katika vyuo vikuu vyake zaidi ya 200 kutokana na kuwa ni chuo kikuu kimoja pekee ndicho kinachofundisha lugha hiyo.Imeeleza kuwa nafasi hizo ni tofauti na zile zinazotolewa na taasisi na mashirika ya Ufaransa ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano uliodumu kwa miaka mingi.Balozi wa Ufaransa nchini, Frédéric Clavier alibainisha hayo katika kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu vya Ufaransa na Tanzania kuendeleza mahusiano katika sekta ya elimu.Kongamano hilo lilishirikisha wanafunzi zaidi ya 900 kutoka vyuo vikuu nchini na Ufaransa na kujadili masuala mbalimbali ikiwemo kupata ajira katika kampuni 40 za uwekezaji na ufadhili wa elimu ya juu.Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amesema kutokana na uusiano wa nchi hizo, Balozi amesema serikali ya Ufaransa imeongeza ufadhili kwa wanafunzi wa Kitanzania kutoka 30 kwa mwaka mpaka 50.Alisema daima marafiki wanazungumza lugha moja na kutokana na uhusiano wa miaka mingi kati ya Tanzania na Ufaransa, imefika wakati wa vyuo vikuu nchini Ufaransa kufundisha lugha ya Kiswahili.“Wakati tunahamasisha Watanzania kujifunza Kifaransa katika nyanja mbalimbali, ni vema vyuo vikuu vya Ufaransa pia vikaanza kufundisha lugha ya Kiswahili ili Wafaransa wengi zaidi waifahamu,” amesema.Alisema kati ya vyuo vikuu 200 nchini humo, kimoja kinafundisha Kiswahili vingine vyote Kiingereza.Kongamano hilo ni fursa ya elimu na ajira kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kupata taarifa ya kozi na mifumo ya elimu Ufaransa ili kufanya tafiti za pamoja.Alibainisha kuwa wanafunzi wanaweza pia kupata ufadhili wa masomo kutoka Ufaransa ikiwemo vyuo vikuu nchini kufahamu kiwango cha wanafunzi wanaowataka kuwaajiri katika kampuni 40 za uwekezaji. | 3 |
TIMU ya Azam FC imelazimishwa suluhu ya bila kufungana na Mbao FC, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza na kuendelea kujiweka katika mazingira magumu kwenye mbio za kuwania ubingwa.Matokeo hayo yamewafanya Azam kufikisha pointi 63 baada ya kucheza michezo 30 katika muendelezo wa ligi hiyo inayoongozwa na Yanga yenye pointi 68 wakicheza michezo.Hiyo ni mechi ya kwanza kwa kocha Abdul Mingange na msaidizi wake, Iddi Cheche kupata pointi moja tangu wakabidhiwe jukumu la kukinoa kikosi hicho baada ya kutimuliwa kwa benchi zima la ufundi la Hans Van Der Pluijm.Mchezo huo ulianza kwa kasi kubwa huku kila timu ikiwa makini wakihofia kuruhusu bao la mapema, ambapo hali hiyo iliendelea hadi mapumziko na kuzifanya timu hizo kwenda katika vyumba vya kubadilishia nguo zikiwa suluhu.Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikifanya mabadiliko ambayo hayakuzaa matunda kwa pande zote.Azam walipata pigo baada ya nahodha wao kupata kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mshambuliaji wa Mbao.Hadi mwisho wa mchezo, timu hizo zilitoshana nguvu kwa kila mmoja kuondoka na pointi moja. | 4 |
TAASISI ya Utafiti ya Wanyamapori (Tawiri) inajivunia kuratibu kongamano la 12 la tafiti za wanyamapori Tanzania wakihusisha watafiti wa ndani na nje ya nchi ambalo litajadili suala la utawala bora wa maliasili na ikolojia ya wanyamapori na mahusiano ya viumbe.Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika jijini Arusha, Desemba 4 hadi 6, mwaka huu likiongozwa na kauli mbiu ijulikanayo “uhifadhi endelevu wa bayoanuai Tanzania.”Akizungumza katika banda la Tawiri lililopo ndani ya Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa (DITF), yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa Dar es Salaam, Mtafiti Jerome Kimaro alisema hatua hiyo ni jambo kubwa kwa Taasisi hiyo na kupitia maonesho hayo wadau wengi wamefahamu suala hilo.Alisema kongamano hilo linalofahamika kama Tawiri Scientific Conference hufanyika kila baada ya miaka miwili na huleta manuf mengi nchini ikiwemo kutangaza vivutio vya kitalii vilivyopo nchini.“Kupitia maonesho haya ya sabasaba wengi wamejiandikisha kushiriki wakiwemo wanafunzi wa vyuo, jambo ambalo litaongeza ushiriki, “ alisema Kimaro na kuongeza kuwa kupitia kongamano hilo mamlaka husika zitapokea mapendekezo mbalimbali, uelewa na hata kuboresha sera na kusimamia utekelezaji wa shughuli za wanyamapori.Alisema pia washiriki katika kongamano hilo watajadili kuhusu magonjwa ya wanyamapori na afya ya mfumo ecosystem... Na hata kuelezwa kwa matokeo ya tafiti mbalimbali.Kimaro alisema maonesho hayo yamekuwa na tija kwao kwani wanaendelea kutoa taarifa za wanyamapori ili kusaidia uhifadhi na utalii.Kadhalika alisema kupitia maonesho hayo wameweza kutoa idadi ya tafiti waliofanya walipo, walikotoka na waendako huku alibainisha kuongezeka kwa idadi ya watanzania wanaoshiriki katika shughuli za kutafiti dhana ambayo ilijulikana ni mataifa mengine pekee (wazungu) ndio yenye uwezo wa kufanya hivyo.Alisema hivi sasa zipo tafiti 126 na watafiti wote idadi yao ikiwa ni 332 huku miongoni mwao watanzania wakiwa ni 119 sawa na asilimia 35.5.Tawiri pekee ina miradi zaidi ya 40. | 3 |
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema kwa sasa kinaelekeza nguvu zake kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwakani wa madiwani, wabunge na Rais.Kimesema hakina mpango wa kufanya maandamano siku ya kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa keshokutwa, kama inavyovumishwa na baadhi ya watu na mitandao ya kijamii. Kwamba baadhi ya watu na mitandao hiyo, wamekuwa wakivumisha hivyo tangu kilipotangaza kujitoa katika uchaguzi huo.Hayo yalielezwa juzi na Mwenyekiti wa Taifa wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alipotoa maazimio ya Baraza Kuu la Uongozi la chama hicho. Baraza hilo lilifanya kikao chake cha kawaida Novemba 13-15 jijini Dar es Salaam.Lipumba (pichani) alidai kutokana na ‘figisu figisu’ zilizojitokeza katika Uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa na kusababisha asilimia 98 ya wagombea wa chama hicho kuenguliwa, kwa sasa wameona ni vyema kuyajenga matawi kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani. “Tunaamini hatua hiyo itatusaidia kudhibiti mpango uliotumiwa katika uchaguzi wa wa serikali za mitaa.Matawi yatatuongezea mtaji wa wanachama katika maeneo yote na hivyo kukifanya chama kuwa na nguvu,” alisema Profesa Lipumba. Alisema CUF imeamua kukaa kimya tangu ilipotoa tamko la kujitoa katika uchaguzi huo. Kwamba kwa sasa inaendelea na mipango yake ya ujenzi wa matawi hayo na siyo kupanga maandamo, kama baadhi ya watu wanavyodai.Profesa Lipumba alisema kama kweli chama hicho, kingekuwa kina nia ya kufanya maandamano hayo, kingefuata utaratibu kiliyowahi kuutumia mwaka 2001, kwa kupita na kutoa taarifa katika matawi yote, lakini pia katika vyombo vya usalama, kama taratibu zinavyotaka. Akizungumzia maazimio yaliyofikiwa, alisema Baraza Kuu limeiagiza Kamati ya Utendaji ya Taifa, kuwasiliana na viongozi wa dini na wadau wengine nchini, kujadili hatma ya taifa kutokana na hali iliyojitokeza katika Uchaguzi wa keshokutwa wa Serikali za Mitaa.Mbali na hilo, Profesa Lipumba alisema Baraza Kuu linawapa pole Watanzania kutokana na kuwa na maisha magumu yasiyo na furaha na hiyo inatokana na taarifa ya Umoja wa Mataifa ya Furaha Duniani ya Mwaka 2019, inayoonesha Tanzania inashika nafasi ya 153, kati ya nchi 156, zilizofanyiwa utafiti juu ya hali ya furaha. Aidha, alisema CUF inaikumbusha serikali kujenga nyumba za Polisi ili wawe na makazi bora. Pia kwamba chama hicho kinataka polisi waruhusiwe kuhamia katika makazi mapya, yaliyopo eneo la Kilongawima na Mikocheni jijini Dar es Salaam. | 3 |
VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kuacha kuwabeba wagombea wa nafasi mbalimbali katika Uchaguzi Mkuu ujao.Wametakiwa kutofanya hivyo kwa kilichodaiwa kuwa wakati wa kufanya kampeni kwa mujibu wa maelekezo ya chama hicho haujawadia. Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mberwa Hamad Mberwa alisema hayo akizungumza na viongozi wa CCM katika semina elekezi kuwanoa watendaji wa chama.Alisema huu si wakati muafaka kufanya kampeni za uchaguzi, ambapo kazi ya chama hicho na viongozi ni kusimamia na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015/2020. Alisema viongozi waliochaguliwa wana kazi ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi pamoja na ahadi za wapigakura ili kukihakikishia chama ushindi mnono katika Uchaguzi Mkuu ujao mwakani.“Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi hawatakiwi kufanya kazi ya kubeba viongozi wanaokusudia kugombea nafasi mbalimbali katika Uchaguzi Mkuu ujao....huu si wakati wa kufanya kampeni za uchaguzi kwani viongozi waliopo madarakani bado wanaendelea kutekeleza ahadi za Ilani ya Uchaguzi,” alisema.Kaimu Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba, Khamis Ali aliwataka viongozi kufanya kazi ya kutafuta wanachama wapya watakaoshika usukani kuongoza nchi. Alisema katika miaka tisa ya uongozi wa Rais Dk Ali Mohamed Shein, mafanikio makubwa yamepatikana ya kuwezesha huduma za jamii, barabara na ujenzi wa shule na hospitali.“Viongozi kazi yetu kubwa ni kuimarisha chama kwa kuingiza wapigakura wapya ambao watailetea ushindi CCM uchaguzi mkuu ujao,” alisema. Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sada Amrani aliwataka wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi na kushiriki uchaguzi ujao.Alisema chama hakina vikwazo kwa wanawake kuwania nafasi za uongozi kuanzia majimbo ya uchaguzi ambapo wanawake wanatakiwa wagombee nafasi katika majimbo ya uchaguzi. “Wanawake wa CCM jitokezeni kugombea nafasi za uongozi kuanzia ngazi za majimbo ya uchaguzi ambapo nafasi za majimbo wasiachiwe wanaume pekee,” alisema. | 3 |
Na Mwandishi Wetu –Dar es Salaam ZIKIWA ni siku chache tangu daladala zipigwe marufuku kusimamisha abiria, ikiwa ni njia ya kukabiliana na corona, Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra) imetoa wito kwa watu binafsi, shule na taasisi zenye mabasi ambayo hayajapangiwa njia kuomba leseni za muda mfupi ili watoe huduma. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Latra, Gilliad Ngewe, watu wenye mabasi ya abiria ambao hawajapangiwa njia wametakiwa kufika ofisi za mamlaka hiyo kuomba leseni kusudi kuanza kutoa huduma hiyo. Hivi karibuni Latra iliagiza mabasi yote yaendayo haraka (BRT) na daladala zote kubeba abiria kulingana na idadi ya viti vilivyopo, ukiwa ni mkakati wa kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona (Covud-19). Pia Latra iliagiza kila chombo cha usafiri kiwe na dawa ya kuua virusi mikononi (hand sanitizer) kabla ya abiria kuingia ndani ya basi asafishe mikono kwa dawa ya kuua virusi mikononi. Ngewe alisema utekelezaji wa agizo hilo ni hatua ya kujikinga dhidi ya virusi vya corona katika vyombo vya usafiri. ” Latra imekutana na wadau wa usafiri na usafirishaji ardhini na kutafakari kuweka mikakati ya kukabiliana na janga hili, wamiliki wote na wafanyakazi wao wanaagizwa kuhakikisha wananyunyizia mabasi yao dawa kila mwisho wa safari. “Pia Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (Tazara) wahakikishe treni zinapulizwa dawa kila mwisho wa safari,” alisema Ngewe. Mbali na hilo, Ngewe alisema kwa magari ya mizigo hayaruhusiwi kubeba abiria yeyote huku akisisitiza elimu juu ya kujikinga na virusi vya corona itolewe ndani ya vyombo vya usafiri kwa kutumia redio na runinga katika magari hayo. “Lakini hatua nyingine, kuanzia sasa haitoruhusiwa watu wanaomsindikiza abiria kuingia katika vituo vya treni au mabasi yaendeyo mikoani,” alisema Ngewe. | 3 |
MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) imesema itafanya uchunguzi ili kubaini sababu za Kampuni ya R& S Inter Trade ya Vingunguti jijini Dar es Salaam, kukutwa na shehena kubwa ya vipodozi vilivyokwisha muda wa matumizi.Meneja wa TFDA wa Kanda ya Mashariki jijini Dar es Salaam, Emmanuel Alfonce alisema hayo alipofanya mahojiano maalumu na gazeti hili kuhusu kampuni hiyo kukutwa na vipodozi hivyo vilivyokwisha muda wake.Chanzo kimoja cha habari kililiambia gazeti hili uwepo wa shehena ya zaidi ya katoni 2,000 za vipodozi vilivyokwisha muda wake katika ghala la kampuni hilo, lililopo Vingunguti jijini Dar es Salaam.Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, kampuni hiyo iliingiza zaidi ya katoni 4,000 za vipodozi vilivyoharibika muda wake katikati ya mwaka jana, lakini baadaye ilibainika kuwa vilikuwa vimekwisha muda wake, ambapo wakaguzi kutoka TFDA waliamuru vipodozi hivyo kuteketezwa.Hata hivyo, pamoja na agizo hilo, ilidaiwa kuwa hadi sasa ikiwa ni zaidi ya miezi sita, bado vipodozi hivyohavijateketezwa, hatua inayodaiwa kuwa inaweza kusababisha udanganyifu kwa vipodozi hivyo kuingizwa sokoni kwa njia zisizo halali.Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja Alfonce alisema pamoja na kufuatilia ili kujua sababu zilizosababisha vipodozi hivyo kushindwa kuteketezwa kwa muda mrefu sasa, lakini pia itafanya uchunguzi kubaini sababu za kampuni hiyo kukutwa na kiwango kikubwa cha vipodozi vilivyokwisha muda wake.“Tutafuatilia kujua ni kwanini kampuni hiyo imeweza kuwa na kiwango hicho ambacho ni kikubwa sana cha vipodozi vilivyokwisha muda wake.“Kuhusu kuviteketeza utaratibu wa vipodozi ni tofauti kidogo na vyakula ambavyo baada ya kuvikamata vikiwa vimeharibika, tunamuamuru aliyekutwa navyo kuvipeleka dampo Pugu chini ya usimamizi wetu.“Kwa vipodozi Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezuia kuvipeleka dampo vikiwa vimekwisha muda wake kwa vile vinaweza kuwa na kemikali zenye athari kwa ardhi na mazingira, kwa hiyo kinachofanyika kwa vipodozi ni kuviteketeza kwa kuvichoma moto na kuna matanuru maalumu ya kuviteketeza,” alisema meneja huyo.Alisema kwa vile wakaguzi wa TFDA walishafika katika maghala ya kampuni hiyo na kuamuru kuteketezwa kwa vipodozi hivyo, watafuatilia ili kuona ni kwanini kazi hiyo haijafanyika hadi sasa.Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Nassoro Abdallah alikiri kuwepo kwa vipodozi hivyo vilivyokwisha muda wake katika ghala la kampuni yake.Hata hivyo Mkurugenzi huyo alikanusha madai kwamba shehena hiyo, imekuwa inapungua bila kujua katoni nyingine zinakwenda wapi, kama ilivyodaiwa na vyanzo vya habari.Alisema ipo shehena kidogo ambayo iliteketezwa, ingawa alishindwa kusema kazi hiyo ilifanyika lini na ilisimamiwa na chombo gani. | 3 |
Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kuwepo kwa mfumuko huo wa bei kumetokana na fahirisi ya bei ya bidhaa mbalimbali kuongezeka hadi 150 mwezi Aprili mwaka huu kutoka 141.59 mwezi Aprili mwaka 2013.Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa NBS Ephraim Kwesigabo, alisema jana kuwa mfumuko wa bei wa mwezi Aprili umeongezeka kutokana na baadhi ya bidhaa za vyakula kuongezeka bei pamoja na bidhaa zisizo za chakula hasa mkaa.Mchele unaelezwa kuwa bei yake imepanda kwa asilimia 3.5, mahindi asilimia 2.5, unga wa muhogo asilimia 4.8, kuku wa kienyeji asilimia 1.3, dagaa asilimia 6.0, samaki wakavu asilimia 7.8, matunda kwa asilimia 1.4 na karanga asilimia 2.6 .Mkaa ambao unaangukia katika kundi la bidhaa zisizo za chakula umechangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa asilimia 4.3, huduma za matibabu asilimia 3.0, dizeli asilimia 4.4 na gharama ya kusaga nafaka nayo iliongezeka kwa asilimia 6.6.Kwesigabo alisema mfumuko wa mwezi Aprili mwaka huu ambao unapimwa kwa kipimo cha mwezi umeongezeka kwa asilimia 0.7 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 0.6 iliyokuwa mwezi Machi mwaka huu.Alisema mfumuko kwa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi umeongezeka hadi asilimia 7.8 mwezi Aprili kutoka asilimia 7.2 ya mwezi Machi mwaka huu.Alipoulizwa sababu ya kuongezeka kwa bei hizo, Kwesigabo alisema "Licha ya kuwa hatujafanya utafiti lakini mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini zimechangia kuwepo kwa mfumuko wa bei."Alisema gharama za usafirishaji wa bidhaa kutoka mashambani kwenda kwenye miji mikuu ya mikoa imeongezeka hali ambayo imechangia kuwepo kwa ongezeko hilo. | 5 |
KOCHA wa timu ya Yanga, Charles Mkwasa amesema ushindi walioupata kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons umewapa nguvu ya kujipanga kuikabili Biashara United katika mchezo utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.Mkwasa alitoa kauli hiyo juzi baada ya kikosi chake kuibuka na ushindi kwa kuifunga Tanzania Prisons bao 1-0 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Samora Iringa, na kupanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi 21. Alisema wanauchukulia mchezo huo kama fainali kwa kuwa ni moja ya timu zinazoonesha ushindani mkubwa kutafuta matokeo hususani kwenye viwanja vya ugenini.“Ninawashukuru wachezaji kwa ushindi tuliopata kwani umetuongezea nguvu ya kujipanga kwenye mchezo wetu unaokuja dhidi ya Biashara United kuhakikisha tunapata matokeo kama haya kujipanga na mchezo wetu wa Januari 4 dhidi ya Simba,” alisema Mkwasa Alisema mchezo uliopita walicheza kwa kiwango cha juu kwa kumiliki mpira na kutengeneza nafasi nyingi katika kipindi cha kwanza lakini wachezaji wake walikosa umakini na kushindwa kumalizia kupata mabao ambayo yangewafanya kumaliza mchezo kipindi cha Kwanza. Alisema kipindi cha pili wapinzani wao walicheza mpira wa nguvu na kupiga vikumbo kuwatoa mchezoni jambo ambalo walifanikiwa lakini alitoa maelekezo kwa wachezaji wake kurudi nyuma kulinda ushindi waliopata kipindi cha kwanza. Naye kocha wa Tanzania Prisons, Mohamed Rishaard ‘Adolf’ alikubali matokeo na kukiri kufanya makosa katika dakika za mwanzo na kufungwa bao jambo ambalo hakulitegemea.“Sina sababu ya kusema uwanja shida lakini kimsingi tulifanya makosa na kuruhusu kufungwa bao la kizamani jambo ambalo sikutegemea, nimekubali kama benchi la ufundi tunaenda kujipanga na ratiba ya mechi zinazokuja kuhakikisha tunapata ushindi” alisema Adolf Alisema matokeo hayo kwa kiasi fulani yamevuruga malengo yao kwani ilikuwa ni kulinda rekodi yao ya bila kufungwa lakini kukosa umakini dakika za mwanzo zimewafanya wafungwe. | 4 |
Agizo hilo lilitolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana mjini Dodoma wakati akiahirisha mkutano wa saba wa Bunge la Bajeti 2017/18. Alimwagiza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe kulivunja.Alisema hawatafumbia macho usimamizi mbovu wa michezo usiojali maslahi ya Taifa. “Serikali imeazimia kuimarisha utendaji kwa vyombo vya michezo nchini ili kila mwenye dhamana awajibike ipasavyo.Haitafumbia macho usimamizi mbovu na utawala wa michezo usiojali maslahi ya Taifa,” alisema. Hatua hiyo inamaanisha kuvunjwa kwa uongozi wa BMT chini ya Mwenyekiti, Dioniz Malinzi, kaka wa Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamal Malinzi aliyeko mahabusu akikabiliwa na kesi akidaiwa kutakatisha mamilioni ya fedha.Majaliwa alimwagiza Waziri Mwakyembe kufanya mapitio na tathmini ya uwepo wa BMT kujiridhisha kama inafaa iwepo au ivunjwe. “Namuagiza Waziri wa Michezo kulipitia Baraza la Michezo kujiridhisha na usimamizi wake wa michezo.Naelekeza Baraza la Michezo la Taifa (BMT) livunjwe, shughuli zake zitafanywa na sekretarieti hadi baraza jipya litakapoundwa,” alisema. Alimpongeza Rais John Magufuli kwa kuunga mkono uendelezaji michezo kwa kujenga uwanja wa kisasa wa kimataifa mjini Dodoma kwa msaada wa nchi rafiki ya Morocco.Alilitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwaendeleza na kuwatunza wachezaji wa timu ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ‘Serengeti Boys’ waliocheza fainali za vijana Afrika Gabon.Aliipongeza Serengeti Boys kwa kuonesha upinzani mkubwa katika mashindano ya soka ya vijana wa chini ya miaka 17 AFCON akisema kwa upande wake timu hiyo ni washindi. “Binafsi nilifuatilia mechi zote za Serengeti Boys.Nikiri kwamba vijana hao wana vipaji na uzalendo wa hali ya juu kwa nchi yao. Kwangu mimi vijana wale ni washindi bila hata kuwapa taji lolote, kwani kanuni za mashindano ndizo zilizowafanya watolewe,” alisema Majaliwa.Serengeti Boys iliondolewa ikiwa na pointi 4 sawa na Niger lakini ikazidiwa kwa tofauti ya mabao iliyofungwa (1-0) zilipokutana na Niger. “Msisitizo wangu kwa TFF ni kuendelea kuwatunza vijana hao na kusimamia klabu za michezo na kuwekeza kwenye soka la vijana ili tujenge timu imara kwa miaka ijayo,” alisema. | 4 |
Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amesema Zanzibar ipo katika mikakati ya kutekeleza uchumi wa buluu, ambayo itaiwezesha kuvuna rasilimali za baharini na kuongeza pato kwa wavuvi.Alisema hayo Malindi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa soko la kisasa kwa ajili ya wavuvi. Dk Shein alisema Zanzibar inayo hazina ya rasilimali za baharini, ikiwemo samaki wakubwa ambao wakivuliwa wataongeza pato la wavuvi.Aliitaja mikakati iliyochukuliwa sasa kuwa ni kununua meli ya uvuvi, itakayokuwa na uwezo wa kuvua eneo la bahari kuu. Alisema serikali imelifufua upya Shirika la Uvuvi (ZAFICO) ambalo litalaratibu shughuli za uvuvi katika ukanda wa eneo la bahari kuu.“Hiyo ndiyo mikakati yetu kuona kwamba tunaingia katika uchumi wa buluu na kutuwezesha kuvuna rasilimali za baharini na kulitumia eneo la bahari kuu kwa uvuvi,” alisema. Alisema boti nyingine nne kwa ajili ya kuvua eneo la bahari kuu, zipo katika hatua za mwisho kuingia Zanzibar.“Tumeagiza boti nyingine nne kwa ajili ya uvuvi wa bahari kuu ili kuona wavuvi wetu wanafaidika na kuvuna rasilimali za baharini kikamilifu,” alisema.Alisema ujenzi wa soko jipya, utawawezesha zaidi ya wavuvi 600 kupata huduma mbalimbali huku akisisitiza usafi utakaozingatia mazingira.“Soko hili litakuwa na hadhi ya kimataifa, kwa hiyo wavuvi na wananchi watakaolitumia wanatakiwa kuzingatia usafi wa mazingira yake.”Alilipongeza Shirika la Kimataifa la Misaada la Japan (JICA) kwa misaada yake, ambayo imelenga kukuza uchumi na ustawi wa sekta ya uvuvi. Mapema Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Mmanga Mjengo Mjawiri aliwataka wavuvi kuacha uvuvi haramu, ambao umesababisha baadhi ya maeneo kukabiliwa na uhaba mkubwa wa samaki na rasilimali zake.“Soko hili tunataka litumiwe kwa ajili ya kuleta samaki na bidhaa zake ambazo zinakidhi thamani na hadhi ya soko,” alisema.Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Misaada la Japan (JICA), Matsuyama Satoru alisema ujenzi wa soko hilo utagharimu Sh bilioni 26.491, ambapo Sh bilioni 22.776 kati ya hizo ni msaada na zitatolewa na (JICA). Katika ujenzi wa soko hilo, Sh bilioni 3.715 zitatolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. | 3 |
Aveline Kitomary, Dar es salaam JUMLA ya Watoto 48 wenye magonjwa ya moyo wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa kufungua kifua
na upasuaji wa tundu dogo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete(JKCI). Matibabu
hayo ya Moyo kwa watoto yamefanywa na madaktari bingwa kutoka Saudi Arabia
wanashirikiana na madaktari wa JKCI katika kambi ya siku ya siku saba
inayofanyika katika Taasisi hiyo ambayo pia yamehusishwa upimimaji wa watoto. Akizungumzia
na MTANZANIA jana jijini Dar es salaam
Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji Angela Muhozya alisema kwa asilimia kubwa ya watoto waliofanyiwa
upasuaji ni wale waliozaliwa na matatizo ya Moyo kama matundu na matatizo ya
mishipa. “Tumeanza
upasuaji kuanzia Jumapili siku hiyo tumefanya upasuaji wa kufungua kifua kwa
watoto watano, Jumatatu tulifanya kwa watoto watano,jumanne watoti wanne na
jana jumatano watoto walikuwa sita. “Katika
upasuaji wa bila kufungua kifua tulianza jumatatu ambapo watoto saba walipata
huduma siku ya jumanne watoto nane na leo Jumatano tunaowafanyia watoto
12,”alibainisha. Kwa upande
wake mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake alifanyiwa upasuaji Rose Msaki alisema
mtoti wake Juniour Mollel alikuwa na tatizo la kuwa tundu moja ambayo ilikuwa
imepitisha damu safi na chafu. “Aliugua
kwa muda wa mwaka na mwezi mmoja tulijua anatatizo la nimonia akiwa na miezi
miwili kuna daktari akaniambia nimlete hapa afanyiwe uchunguzi wa moyo sasa
wamefanyiwa upasuaji na anaendelea vizuri naishukuru serikali yetu na ya Saudi
Arabia,”alieleza. | 0 |
TANGU kuanza kuadhimishwa kwa Siku ya Kimondo duniani idadi ya Watanzania wanaofi ka kutalii eneo la kimondo, katika eneo la Mbozi mkoani Songwe imeongezeka kutoka watalii 1,300 hadi kufi kia watalii 3,580 ambalo ni ongezeko la zaidi ya na asilimia 80 na idadi ya wageni toka nje ya nchi ikiwa 116. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kituo cha Kimondo Mbozi jana, Paul Nyello alipokuwa akizungumza na msafara wa mgeni rasmi Mkuu wa Nkoa wa Mbeya, Albert Chalamila aliyemwakilisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Harison Mwakyembe wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya kimondo kitaifa ambayo kilele chake ni leo. Nyello alisema tangu kuanza kwa maadhimisho hayo mwaka jana yamechangia kuwahamasisha wananchi kuanza kujitokeza kwa wingi kutembelea eneo hilo na kwamba hamasa imesaidia kuongeza uelewa kwa wananchi na sasa wanajitokeza kwa wingi tofauti na zamani idadi ya watanzania waliokuwa wanafika ilikuwa ndogo na kuifanya eneo hilo kuonekana halina maana yoyote.“Siku za nyuma hapa palikuwa na ukame wa watalii, tulikuwa tukipokea zaidi wageni kutoka nje ya nchi ambao idadi yao hata hivyo bado ni ndogo, bila shaka kadiri tutakavyokuwa tunaendelea kukitangaza kimondo itaongezeka sambamba na idadi ya watanzania ambayo sasa imeongezeka,” alisema Nyello. Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alishauri kukitumia na kukienzi kimondo kwa kuboresha miundombinu ya maeneo hayo na kuibua fursa nyingine ambazo zitawanufaisha zaidi wazee na wananchi wa eneo hilo la Ndolezi.“Wakati Arusha mzee aliyegundua madini ya Tanzanite alipewa zawadi , imefika wakati sasa na sisi huku wazee wetu na wananchi wa eneo hili wanufaike kwa kuwaboreshea mandhari na kuwajengea hata shule kubwa au hospitali kubwa ambayo itakuwa kumbukumbu muhimu kwa wakazi wa kata hii, wilaya, mkoa na Taifa kwa ujumla,” alisema Chalamila . Alisema mikoa saba ya Nnyanda za Juu Kusini itaendelea kukitumia kimondo kuutangaza mkoa na kuibua fursa nyingine za uwekezaji zilizopo mikoa yote saba ya nyanda hii kama vile kwenye kilimo, madini na utalii kutokana na mikoa hiyo kusheheni vivutio vingi. | 3 |
WANANCHI wanaoishi Kata ya Murriet juu ya Kituo cha Afya cha Murriet wamelalamikia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Auwsa) kwa kutopata huduma ya maji zaidi ya mwezi mmoja na nusu sasa. Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti mwishoni mwa wiki, wananchi hao walisema awali walipounganishiwa maji yalikuwa yakitoka siku za Jumatatu usiku hadi Jumanne asubuhi lakini katika kipindi cha Juni, Julai na Agosti hakuna maji yanayotoka.Mmoja wa wananchi hao, Julieth John alisema inashangaza mabomba hayatoi maji lakini ankara zinakuja kubwa. “Usiku tunaacha mabomba wazi ili tujue kama maji yanatoka au la lakini tangu wakati huo hadi leo hii (jana) hakuna maji, sisi wananchi wa karibu na kituo cha afya kwa juu hatupati maji kwenye mabomba, tunaishia kununua kwenye bajaji kwa Sh,10,000 au kwenda kuchota kwenye bomba la kijiji kwa umbali kidogo,” alisema. Kwa upande wake, Salome Lucas alihoji kuna faida gani ya kuvuta mabomba yasiyotoa maji halafu ankara zinakuja kubwa? “kwa nini kwa wengine maji yatoke lakini hospitali kwa juu hakuna maji wakati mwingine hata hicho kituo cha afya kinakosa maji? “Wasoma mita wao wanadai bomba likiwa wazi maji yanapotoka kwa wengine upepo unasoma maji yametoka wakati maji hayatoki, kuna shida gani huko Auwsa kama maji ni madogo waseme. Na kwa nini hawatuongezei maji huku juu kama zamani hizi ankara nani atalipa wakati hatujapata maji, huku ni kukusanya mapato bila kuzingatia haki za watumiaji wa maji,”alisema. Aliomba Bodi ya Auwsa kutembelea eneo la Murriet ili waone wananchi wanavyoteseka kwa kukosa huduma ya maji, huku kukiwa hakuna majibu ya matumaini kutoka Auwsa. Alieleza kuwa walipoilalamikia mamlaka hiyo waliambiwa kuwa kuna bomba limekatwa Burka hivyo wapo kwenye matengenezo .Naye, Msemaji wa Auwsa, William Shayo alisema tatizo la ukosefu wa maji linatokana na mamlaka hiyo kubadilisha miundombinu katika mradi mkubwa wa maji unaoendelea hivi sasa kwa Jiji la Arusha na kutoa rai kwa wananchi kuhifadhi maji vizuri kwani tatizo hilo litandelea hadi Oktoba mwaka huu. | 3 |
WAKALA wa Serikali wa Mtandao nchini umebuni mfumo shirikishi wa kusimamia Shughuli na Rasilimali za Taasisi (ERMS) ambao unaunganisha shughuli za taasisi kuwa katika mfumo mmoja ambao utawezesha kufuatilia, kusimamia ukaguzi na tathimini ya utekelezaji kwa ufanisi.Katika mkutano wake na waandishi wa habari Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Serikali Mtandao, Dk Jabiri Bakari amesema wameamua kutengeneza mfumo wa ERMS ambao ni dirisha moja linalounganisha shughuli zote ndani ya taasisi ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi na utoaji huduma bora kwa umma.Dk Bakari amesema ERMS ina moduli 18, zinazounganisha shughuli mbalimbali za utendaji kazi ambazo zinategemeana na kuwezesha kubadilishana taarifa miongoni mwa Idara, vitengo na kusimamia rasilimali kama vile watu fedha na vitendea kazi.Amesema mfumo huo pia unawezesha ushughulikiaji wa miamala kutoka idara moja hadi nyingine kama vile ankra za bidhaa na huduma, mapato na majukumu ya watumishi ikiwemo ufuatiliaji wa miradi.“Inaweza kutoa pia hali ya matumizi ya fedha, taarifa zinazosaidia katika upimaji wa utendaji wa watumishi katika utoaji wa matumizi sahihi,” amesema Dk Bakari.Pia ERMS inaweza kuunganishwa na kubadilishwa taarifa za mifumo mingine mikuu ya serikali kama vile Mfumo wa Mkuu wa Uhasibu, Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Rasilimali Watu, mfumo wa malipo ya serikali ya kielektroniki, mfumo wa barua pepe serikalini na mfumo wa ofisi mtandao.Akieleza mifumo mingine iliyotengenezwa na Wakala katika utekelezaji wa jitihada za Serikali Mtandao nchini, alisema mifumo hiyo kuwa ni pamoja na kuhusishwa kwa iliyokuwa tovuti ya serikali na kuwa tovuti kuu ya serikali.Amesema kutokana na hilo hivi sasa kazi za mtandao zitakuwa zikifanyika kwa ufasaha zaidi ikiwemo kwa ufanisi kutokana na kwamba imerahisishwa.Dk Bakari amesema baada ya kubuni mfumo huo kila kitu kitakwenda sawa katika utendaji kazi wa mtandao kutokana na mfumo huo mpya ambao umebuniwa ili kusaidia kurahisisha kazi zao za kila siku.Amesema mfumo huo ambao umetengenezwa kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango ambao ni wasimamizi wakuu, ni mfumo wa malipo ya serikali kwa njia ya kielektroniki ambao unalenga kuongeza udhibiti katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato serikalini. | 3 |
KAMPENI ya kuwastiri Watoto wa kike kupata nguo za ndani (chupi na sidiria), imezinduliwa jana jijini Dar es Salaam kwa lengo la kusaidia watoto 1,000 wa mkoani Lindi na Arusha hususani wilayani Karatu.Kampeni hiyo ya siku 40 inaendeshwa na mradi wa Girls in Action Initiative iliopo chini ya Kampuni ya Christom Solution.Akizungumza na wandishi wa habari leo Ijumaa, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Miriam Lukindo alisema walifanya utafiti katika mkoa wa Lindi na Karatu kubaini changamoto zinazowakabili Watoto wa kike ukiachilia ile ya taulo maalum ‘Pads’.Lukindo alisema kuwa utafiti huo walifanya kwenye baadhi ya shule za msingi mbali na kugawa taulo lakini walibaini kuna changamoto kubwa ya Watoto kukosa nguo za ndani.‘Karatu kuna shule tulizotembelea, kati ya watoto 400, watoto wawili tu ndio wamevaa nguo za ndani, wengine wote hawana nguo za ndani, ni changamoto kubwa.“Changamoto zaidi inawakabili pale ambapo wanaingia kwenye siku sawa, kuna mmoja alituambia yeye anatumia gunzi la mahindi kujistiri kipindi cha hedhi.“Anachofanya anachukua pads, anaiweka juu ya gunzi kisha anajiweka huko chini na kuibana na miguu yake, kwa hiyo kipindi cha hedhi mabinti wengi hawaendi shule na hii inawafanya washuke kimasomo.Naye mhamasishaji katika kampeni hiyo iliyopewa jina la ‘Sadaka Ghandi ‘Ant Sadaka’ alisema baadhi ya watoto wa kike kuanzia umri wa miaka 15 hawapendi miili yao kutokana na changamoto zinazowakabili kiasi cha kuwafanya washindwe kujiamini.“Tuwakoe watoto kupata vishawishi vya kupewa pewa pesa ili wakidhi mahitaji yao, changamoto kwa watoto wengi vijiji ni nguo za ndani na taulo za kike, tuungane kwa pamaja katika kampeni hii kwa kuchangia shilingi 1,000 tu kwenye namba 0677 069428,” alisema Sadaka. | 3 |
KLABU ya Yanga imesema inaamini usajili wa wachezaji 26 iliofanya msimu huu utarejesha matumaini ya kufanya vizuri kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Ligi Kuu soka Tanzania Bara.Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Dismas Ten amewaeleza waandishi wa habari kuwa, tayari wamemaliza usajili na sasa wanaendelea na maandalizi mkoani Morogoro.Amesema mpaka sasa ni mchezaji mmoja wa kimataifa hajawasili ambaye ni Mnamibia Sadney Urikhob mwenye matatizo ya kifamilia, lakini atawasili wakati wowote kwa kuwa kibali chake kimeshawasili nchini.“Kwa usajili tuliofanya ni imani tutakuwa na kikosi imara kitakachoshindana kimataifa na kutuwezesha kufanya vizuri msimu huu kuliko huko tulikotoka,” alisema.Ten amesema wanatarajia kucheza mechi nne za kirafiki za kujipima nguvu ambapo moja itachezwa Dodoma dhidi ya Dodoma FC Julai 27, mwaka huu na tatu zitachezwa Morogoro kuanzia Julai 15, mwaka huu.Kiongozi huyo aliwatoa hofu wanachama na mashabiki wa klabu hiyo kuhusu sherehe yao ya wiki ya wananchi ‘Kubwa Kuliko’akisema itafanyika isipokuwa tarehe itabadilika kutokana na kuingiliana na mechi za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndnai, Chan.Alisema sherehe hiyo itafanyika uwanja wa taifa na kucheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki katika tarehe itakayotangazwa na Kamati ya Utendaji.Katika hatua nyingine, alizungumzia maandalizi ya kikosi cha timu ya wanawake Yanga Princess akisema usajili unaendelea na tayari wameshasajili zaidi ya wachezaji 13.Pia, kuhusu Kocha Edna Lema kutua Jangwani kwa ajili ya kuwanoa Yanga Princess alisema kuna mazungumzo yanaendelea bado hayajakamilika hivyo kama watakubaliana basi itatolewa taarifa. | 4 |
PATRICIA KIMELEMETA-DAR ES SALAAM MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imebatilisha kifungu
cha sheria cha namba 7(1) na 7(3) kinachowaruhusu wakurugenzi wa majiji,
manispaa na halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi nchini. Kesi hiyo namba 8/2018, awali ilikuwa inasikilizwa
na jopo la majaji watatu, wakiongozwa na aliyekua Jaji Kiongozi, Ferdinand
Wambari, ambaye kwa sasa amehamishiwa Mahakama ya Rufaa, Jaji Rehema Sameji,
ambaye pia yupo Mahakama ya Rufaa na Jaji Temba amestaafu. Kesi hiyo ambayo mjibu maombi alikuwa ni Mwanasheria
Mkuu wa Serikali (AG), ilifunguliwa na Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), Bob Wangwe, aliyekuwa akiwakilishwa na Wakili Fatma Karume
(ambao ndio waleta maombi) na walikuwa wanapinga kifungu cha sheria ya vyama
vya siasa kinachotumiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwateua wakurugenzi
hao kuwa wasimamizi wa uchaguzi. Akisoma hukumu hiyo mahakamani hapo jana, Jaji
Atuganile Ngwala, alisema kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, kifungu namba 7(1)
na 7(3) ni batili kwa sababu kinatoa nafasi kwa wateule wa Rais ambao pia si
waajiriwa wa NEC kusimamia uchaguzi. Alisema kifungu cha 7(1), kinasema kuwa kila
Mkurugenzi wa Jiji, Manispaa na Halmashauri anaweza kusimamia uchaguzi wakati
viongozi hao ni wateule wa Rais na si waajiriwa wa NEC wakati Katiba inasema NEC
inapaswa kuwa huru na haki. Alisema kutokana na hali hiyo, kifungu hicho
kinakinzana na Katiba mama ambayo inasimamia nchi. Alisema lakini pia kifungu cha 7(3) kinasema kuwa
NEC inaweza kuteua mtu yeyote kuwa msimamizi wa uchaguzi bila ya kuainisha ni
mtu wa aina gani. Alisema lakini Katiba inasema kuwa mtu yeyote aliyekuwa
msimamizi wa uchaguzi hapaswi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Alisema kutokana na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani
hapo na upande wa waleta maombi, vimeonyesha pasi na shaka kuwa wasimamizi wa
uchaguzi wana masilahi na wateule wao. Alisema kutokana na hali hiyo, mahakama imeona kuwa
vifungu hivyo ni batili na kwamba havifai kutumika wakati wa kusimamia uchaguzi. “Mahakama imebatilisha vifungu vya Sheria ya
Uchaguzi namba 7(1) na 7(3) kutokana na NEC kuteua wakurugenzi wa Jiji,
halmashauri na manispaa kuwa wasimamizi wa uchaguzi wakati ni wateule wa Rais
na si waajiriwa wa NEC,” alisema Jaji Ngwala. NJE
YA MAHAKAMA Akizungumza nje ya mahakama, Wakili Fatma, alisema
hukumu hiyo ni ya kihistoria baada ya mahakama kubaini vifungu namba 7(1) na
7(3) kuwa ni batili kutumika katika sheria ya uchaguzi. Alisema kutokana na sababu hiyo, inaonyesha wazi
kuwa miaka yote wananchi walikuwa wanasimamiwa uchaguzi na viongozi wasio
sahihi. “Miaka mingi tulikua tunapiga kelele kuhusiana na
udhaifu wa baadhi ya vifungu katika sheria ya uchaguzi kuwa ni batili na kwamba
vinaegemea kuwalinda viongozi wa CCM, sasa mahakama imeona hiyo na kuwa vifungu
hivyo havifai, pia vifutwe au Serikali ipeleke muswada wa mabadiliko ya Sheria
ya Uchaguzi bungeni ili vibadilishwe,” alisema Fatma. Alisema katika kesi hiyo, walipeleka vielelezo vya
kuonyesha wakurugenzi 74 ambao ni wanachama wa CCM, wamevalia sare cha chama
hicho na wao ndio wasimamizi wa uchaguzi, wakusanyaji wa makaratasi ya
uchaguzi, wapanga matokeo na watangazaji wa matokeo, jambo linaloonyesha wazi
kuwa hawawezi kutangaza matokeo sahihi bila ya kulinda masilahi ya chama chao. Alisema kitendo hicho kinawanyima haki vyama vingine
kupata mshindi kwa sababu anayesimamia uchaguzi tayari ana mgongano wa masilahi
na chama chake. Alisema kutokana na hali hiyo, kila mwananchi ana
haki ya kwenda mahakamani kudai haki pale anapoona kuna ukiukwaji wa sheria
katika maeneo tofauti. Naye Wangwe aliishukuru mahakama kusimamia haki
katika kesi hiyo na kutoa hukumu inayoonyesha wazi kuwa imetenda haki. “Katika hili lazima tuishukuru mahakama kwa
kusimamia na kutoa hukumu ya haki, kwa sababu ma-DED siku zote wamekuwa
wakilinda masilahi ya waajiri wao kwa kutangaza matokeo yasiyo sahihi katika chaguzi
mbalimbali. | 3 |
Timu hizo zilikwenda kujichimbia sehemu tofauti kujiandaa na mechi hiyo ambayo Yanga ilikuwa Mbeya na Azam ilikuwa Zanzibar.Azam iliwasili jana mchana na kwenda moja kwa moja kambini kwao Chamazi na Yanga ilitarajiwa kuwasili jana jioni na ambapo itajichimbia kwenye moja ya hoteli za Dar es Salaam.Zikiwa Zanzibar na Mbeya, timu hizo zilicheza mechi za kirafiki na timu tofauti na zote zilipata matokeo mazuri.Akizungumza na gazeti hili juzi kocha wa Yanga, Van de Pluijm alisema anashukuru kambi hiyo ya takriban wiki moja imeimarisha kikosi chake.“Tumecheza mechi kadhaa tukiwa huku (Mbeya) na kupata nafasi ya kuangalia kikosi changu, naamini kimeimarika na tupo tayari kucheza na Azam,” alisema Pluijm.Kwa upande wa Azam, kocha wake Stewart Hall alisema timu yake imeiva vya kutosha kucheza na Yanga na kuifunga Jumamosi.“Vijana wangu wako kwenye hali nzuri, matatizo ya umaliziaji kwenye safu ya ushambuliaji yamepungua lakini hayanizuii kufanya vizuri katika mechi zangu,” alisema.Alisema anaamini mechi ya Jumamosi itakuwa ngumu kwani Yanga ni timu kubwa na ina kikosi kizuri pia lakini wamejiandaa kucheza nacho.“Mechi itakuwa ngumu lakini hatuiogopi Yanga, tutacheza nayo na naamini matokeo yetu yatakuwa mazuri,” alisema.Mechi hiyo inatarajiwa kuwa ya vuta nikuvute kutokana na timu hizo kusumbuana mara kwa mara zinapokutana.Msimu uliopita pia zilikutana kwenye mechi ya ngao ya jamii ambapo Yanga ilishinda mabao 3-0.Mara ya mwisho zilikutana mwezi uliopita kwenye mechi ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Kagame ambapo Azam ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 na baadae kutwaa ubingwa kwa kuifunga Gor Mahia kwenye fainali.Katika ligi ya msimu uliopita, timu hizo zote zilitoka sare ya mabao 2-2 katika mechi ya kwanza na mechi ya pili Yanga ilifungwa mabao 2-1. | 4 |
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM
ULAJI wa nyama choma na chipsi umetajwa kuwa ni miongoni mwa sababu zinazochochea watu wengi hasa vijana kupata shinikizo la juu la damu.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dk. Pedro Pallangyo, alipozungumza katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili.
Dk. Pallangyo alisema vyakula hivyo huchochea hali hiyo kutokana na matumizi makubwa ya mafuta yanayotumika kuviandaa na chumvi nyingi inayotumika wakati wa kula.
“Jinsi vyakula hivyo vinavyoandaliwa mafuta mengi hutumika na wakati wa kula watu hupendelea kuweka chumvi nyingi, jambo ambalo ni kosa. Ulaji huu si mzuri kiafya,” alisema.
Dk. Pallangyo ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Utafiti na Mafunzo wa JKCI alisema katika miaka ya nyuma idadi kubwa ya watu katika nchi zilizoendelea ndiyo walikuwa wakipata tatizo hilo lakini sasa idadi kubwa inagundulika katika nchi zinazoendelea.
Alisema mbaya zaidi watu wanaokutwa na tatizo katika nchi zinazoendelea ni wale walio katika umri wa uzalishaji.
“Katika nchi zilizoendelea wastani wa umri wa watu wanaokutwa shinikizo la damu ni wale walio juu ya umri wa miaka juu ya 50 na kuendelea.
“Lakini kwa upande wa nchi zinazoendelea, hasa zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara, Tanzania ikiwamo, picha ni tofauti. Huku wanaokutwa na tatizo ni wenye umri wa miaka 35 hadi 45, yaani kwa wenzetu ugonjwa huu unajulikana kwamba ni wa watu wazima huku kwetu ni ugonjwa wa vijana,” alisema.
Pia alisema tafiti zinaonesha magonjwa ya moyo yanachangia theluthi moja ya vifo vyote vinavyotokea duniani na zaidi ya asilimia 50 ya vifo hivyo vinatokana na shinikizo la juu la damu.
“Utafiti mmoja uliowahi kufanywa katika nchi 23 Barani Afrika, Tanzania ikiwamo ulionesha shinikizo la damu ni sababu ya moyo kushindwa kufanya kazi na kusababisha vifo vya ghafla,” alisema.
Dk. Pallangyo alisema katika nchi hizo ilionekana asilimia 86 ya magonjwa yote ya moyo yanatoka na shinikizo la damu.
“Hapa JKCI kwa miaka mitatu iliyopita tumeweza kufanya utafiti mbalimbali, utafiti huo ulihusisha watu waliopo kwenye jamii na wagonjwa waliolazwa wodini, kwenye jamii asilimia kati ya 42 hadi 56 ya wagonjwa wote tuliowapima walikutwa na shinikizo la juu la damu.
“Asilimia 35 hadi 47 ya wagonjwa waliokuwa wodini wengi mioyo yao ilikuwa imeshindwa kufanya kazi na kusababisha shinikizo la damu,” alisema.
| 3 |
MIRADI 47 ya uwekezaji imeibuliwa na kuanza kutekelezwa kupitia Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (LIC) inayotekelezwa katika halmashauri za mikoa wa Dodoma na Kigoma.Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dk Charles Mhina ameyasema hayo wakati wa kuelezea mafanikio ya mradi huo ambao ulisainiwa Januari mwaka 2015.Amesema miradi hiyo yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 7.019 na kunufaisha watu 18,896 kati ya hayo wanawake ni 6,586 na wanaume 12,310.Dk Mhina amesema miradi hiyo imelenga katika kuboreshaji wa miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji, miundombinu ya masoko, minada, machinjio, utafiti wa vyanzo vya maji na viwanda vidogo."Pia kupitia mradi huu wafugaji na wakulima wapatao 1,500 wamejengwa uwezo kwa kupatiwa mafunzo ya ujasiliamali, kuaandikia maandiko ya miradi na kuwaunganisha na taasisi za fedha kwa ajili ya kujipatia mikopo ili kukuza mitaji yao.Alisema pia wamekarabati cha kutuo cha mafunzo ya kilimo na ufugaji kibiashara kwa nadharia na vitendo kwa vijana na wanawake cha Kibakwe Resource Center katika halmashauri za Mpwapwa ambapo wanawake na vijana wapatao 250 wamepata mafunzo.Dk Mhina amesema pia umewezesha kujengwa kwa vituo 13 vya utoaji huduma za biashara na uwekezaji kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 1.45 ambavyo vimepunguza urasimu wa utoaji wa huduma za biashara na uwekezaji na kuongeza idadi za biashara na mapato ya halmashauri."Kwa sasa mradi unaandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi, upimaji na utoaji wa hati katika miradi mikubwa ya uzalishaji kupitia kilimo cha umwagiliaji na makazi katika halmashauri za Wilaya za Kasulu na Uvinza mkoani Kigoma na zile za Bahi na Kondoa mkoani Dodoma.Ameongeza: "Kukamilika kwa mradi huu unaogharimu zaidi ya Sh milioni 596.33 na tunatarajia wakulima na wafanyabiashara zaidi ya 9,266 watanufaika."Kuhusu eneo la kuboresha miundombinu ya ukusanyaji wa mapato, Dk Mhina amesema LIC wamewezesha kununuliwa kwa mashine za kielektroniki za kukusanya mapato (POS) 235 kwa thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.95.Amesema fedha hizo zimechangia ongezeko la makusanyo kwenye halmashauri za Mkoa wa Kigoma kwa asilimia 88 katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba 2018 na kwa asilimia 130 kwa Mkoa wa Dodoma."Katika eneo hilo mradi umeiwezesha OR-Tamisemi kukamilisha maandalizi ya mwongozo wa usimamizi wa ukusanyaji wa mapato katika mamlaka za serikali za mitaa," amesema.Dk Mhina alisema pia wamefanikiwa kuanzishwa na kuendelezwa kwa mabaraza ya biashara ya wilaya zote za Dodoma na Kigoma. | 5 |
Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti, baadhi ya maofisa wa migodi ya madini nchini walisema kuna changamoto kadhaa ambazo zimechangia wawekezaji katika sekta ya madini kutowekeza kwenye utafutaji wa madini jambo ambalo linaweza kuifanya sekta hiyo kufa au kudumaa.Mwenyekiti wa Chama cha Madini na Nishati, Balozi Ami Mpungwe alisema kuna haja kubwa ya serikali kukutana na wawekezaji wa madini kwa sababu kuna kushutumiana na kulaumiana kila upande jambo ambalo linaweza kutatuliwa kwa mazungumzo.Akizungumza mara baada ya mjadala ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi kuahirishwa kutokana na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini pamoja na Mamlaka ya Mapato (TRA) kutofika kwenye mkutano huo licha ya kuthibitisha kushiriki, Mpungwe alisema mkutano huo ulikuwa muhimu kwa faida ya wawekezaji na serikali.“Sisi wadau wa madini tulialikwa na Uongozi Institute na kama inavyoonyesha Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ndiye aliyetakiwa kufungua mkutano huu, lakini hakufika na pia hakukuwa na mtu kutoka TRA kwa hiyo hii imefanya majadiliano haya yakwame,” alisema Balozi Mpungwe.Alisema wadau kwenye sekta ya madini wana kilio kikubwa ambacho suluhisho la uwekezaji wa sekta hiyo ni serikali kukaa na wawekezaji na kusikia malalamiko yao.“Tungepata nafasi ya kuzungumza na kila mtu angetoa malalamiko yake, kutofanyika kwa mkutano huu ni tatizo kubwa,” alisema.Alisema kwenye uwekezaji wa madini kunategemeana na sera, sheria, kanuni na mfumo wa kodi uliopo ambao alisema kwa sasa kuna changamto katika mambo hayo ambazo zinalalamikiwa na wawekezaji na wanapaswa kuzungumza na Serikali ili kuzitatua.“Hata kule kwenye migodi kwa sasa hakuna usalama, kuna uvamizi mkubwa unafanywa na wachimbaji wadogo katika maeneo ambayo yanamilikiwa kwa wawekezaji, hili nalo ni tatizo kubwa ambalo linawapa woga wawekezaji wengi,” alisema Balozi Mpungwe.Alisema mazingira ya usalama katika migodi kwa sasa unatisha na hiyo hatua hiyo imefanya shughuli za utafutaji wa madini kupungua kwa kuwa kuna mambo mengi ambayo serikali imeyabadilisha ambayo hayawavutii wawekezaji tena.Naye Makamu Rais wa Kampuni ya Accacia, Deo Mwanyika alisema shughuli za utafutaji madini zimepungua kwa sababu mwekezaji yeyote hawezi kutupa mtaji wake kutafuta madini wakati mazingira ya uwekezaji sio rafiki.“Sisi wawekezaji tunasema wazi kuwa mazingira ya uwekezaji katika sekta ya madini sio mazuri, licha ya juhudi za serikali kutaka kuneemeka na sekta hii,” alisema Mwanyika na kuongeza kuwa changamoto ziko kwenye sera na mashindano yaliyopo kati ya wachimbaji wadogo na wachimbaji wakubwa.Pia alisema kitendo cha wachimbaji wadogo kuvamia maeneo ya migodi mikubwa kinawaogopesha wachimbaji wakubwa kuendelea kuwekeza katika utafutaji wa madini kwa sababu hawajui hali ya usalama huko mbeleni itakuwaje.“Sheria ya madini ni nzuri sana kwani inaifanya sekta hii ya madini kuwa sawa na sekta zingine, kwa hiyo tunachotakiwa kufanya kama nchi ni kuweka vivutio kwa wawekezaji katika sekta hii,” alisema Mwanyika. | 5 |
KAMPUNI ya Vodacom katika mwaka huu wa fedha ulioishia Machi 31, imefanikiwa kuongeza mapato yake ya huduma hadi kufikia Sh trilioni moja, sawa na ongezeko la asilimia 5.4.Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Hisham Hendi, ongezeko la mapato hayo limetokana na mapato kukua katika huduma za M-Pesa, huduma za data na SMS.Akizungumza na waandishi wa habari jana mkurugenzi huyo alisema kampuni hiyo imeendelea kushika nafasi ya kwanza katika utoaji wa huduma za mawasiliano na fedha nchini.Alieleza kuwa Vodacom imefanikiwa kufikia wateja milioni 14.1 ambao ni sawa na ongezeko la asilimia 9.6, ikiongeza nafasi yake katika soko, hadi kufikia asilimia 32.4.“Kukua kwa huduma ya M-Pesa kumeendelea kuwa chachu ya uvumbuzi wenye kuboresha ujumuishi katika huduma za kifedha kupitia mifumo kama vile ‘Lipa kwa Mpesa’ ambayo inarahisisha malipo na kuwawezesha Watanzania kujipatia kipato,” alieleza.Alisema katika mwaka uliopita, upanuzi wa huduma za M-Pesa umewezesha wateja wapya 620,000 kufanya miamala kwa njia ya simu.Huu ukiwa ni ukuaji chanya wa wateja kwa asilimia 9.7 wanaotumia huduma hiyo.Alifafanua kuwa mapato yatokanayo na huduma ya MPesa yalikua kwa asilimia 14.5 na kufikia Sh bilioni 333.5.5.“Uhodari wetu kama mtoaji huduma za kifedha kwa njia ya simu ukifika asilimia 38.6 sawa na watumiaji milioni saba wa M-Pesa wanaofanya miamala inayofikia Sh trilioni 4.1 kwa mwezi.”Hendi alisema kupitia M-Pesa, Vodacom imekuwa ikiunga mkono jitihada za serikali katika kujenga uchumi imara wenye ushindani na hivyo kuweka rekodi kubwa ya wafanyabiashara 11,000 waliofanya miamala kufikia Sh trilioni 1.1 katika mwaka uliopita.Ukuaji pekee wa asilimia 186.0. Alisema kukua kwa mawasiliano kumewaleta watu pamoja na kuifanya kampuni hiyo ya Vodacom kuweka huduma za kidigitali katika maisha yao na kuwawezesha kujenga maisha bora ya baadaye.“Hii imedhihirishwa kupitia data ya mapato yaliyokua kufikia Sh bilioni 167 sawa na ukuaji wa asilimia 17.9 huku hatua za kudhibiti kushuka kwa mapato ya sauti zimeendelea kuonesha mafanikio,” alisema.Alifafanua kuwa, ingawa ukuaji wa mapato katika data yanatia hamasa, lakini ili kuweza kutoa mchango katika Pato la Taifa (GDP) na sekta ya afya kwa ujumla, ni muhimu kushughulikia gharama za data kutokana na kiwango cha sasa cha data kuwa cha gharama ya chini.Alisema Tanzania ndio nchi inayoongoza kuwa na data zenye gharama ya chini. Hali hiyo inaifanya kampuni hiyo ishindwe kuwekeza katika miundombinu na teknolojia katika kuendelea kuwaunganisha watanzania.“Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Takwimu (NBS), kufikia mwaka 2030, asilimia 50 ya idadi kamili ya watanzania watakuwa wenye umri chini ya miaka 18. Mgawanyo huo wa idadi ya vijana ni kiashirio kwa Vodacom kuendelea kuwekeza katika mtandao wake,” alieleza.Mkurugenzi huyo alisema mwaka huu, kampuni hiyo ilifanya uwekezaji mahususi wa kiasi cha Sh bilioni 171.4 kukuza uchumi wa nchi na kuwawezesha wateja kupata huduma ya 4G na 4G+ katika majiji makubwa, kuimarisha na kuboresha mtandao ili kuwawezesha wateja kufurahia data. | 5 |
VYOMBO vya habari na jamii kwa ujumla wameaswa uhuru wa habari usitumiwe kama kichochoro cha baadhi ya watu kutukana na kudhalilisha wengine, wakiwemo viongozi.Mwito huo ulitolewa bungeni wakati wa kujadili bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iliyowasililishwa mwishoni mwa wiki na Waziri Harrison Mwakyembe na kupitishwa jana.Kabla ya wabunge kuidhinisha na kupitishia wizara hiyo bajeti ya Sh bilioni 30.8 kwa mwaka ujao wa fedha, suala la uhuru wa habari lilijadiliwa na wabunge wengi na kisha na Waziri Mwakyembe kutolea hoja ufafanuzi akisisitiza kuwa hakuna uhuru usiokuwa na mipaka.Miongoni mwa waliozungumzia suala hilo ni Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye katika kufafanua juu ya hoja ya Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema) aliyekuwa akituhumu serikali, Spika wa Bunge, Job Ndugai alikumbusha wabunge kuwa kigezo cha uhuru wa maoni, wao pia wamekuwa wakitukanwa.“Uhuru wa kutoa maoni si kwamba ukishakuwa mwanasiasa unatukanwa na kusingiziwa na kila mtu. Hivi wewe ukitoa maoni yako ukapinga jambo, ukafafanua jambo utagombana na nani?“Tuwafundishe vijana namna ya kutoa maoni yao badala ya kutumia uhuru wa habari kama kichochoro cha kutukana na kudhalilisha. Watu wana utamaduni wao na heshima unakuta kitoto kidogo kinatukana.“Unapotaka kuiambia serikali lazima uiambie kwenye utaratibu fulani. Kuwa kiongozi ndio utukanwe tu... Nawaonea huruma sana wabunge mnatukwanwa sana,” alisema Ndugai na kusisitiza jukumu la malezi kwa watoto watambue namna bora ya kukosoa. Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) alisisitiza kuwa hakuna nchi isiyokuwa na sheria.“Huwezi kusimama kuwa mimi ni mwandishi wa habari utukane useme kwa sababu una uhuru wa habari. Hata huko kwa wakubwa (nchi zilizoendelea) hakuna mtu anayeweza kuandika akatukana serikali au viongozi... uhuru una mipaka yake, haiwezekani.”Akirejelea hoja za baadhi ya wabunge hususani wa upinzani waliotaja magazeti kadhaa ikiwamo Tanzanite kuwa yanaandika habari za uchochezi na uongo, Nkamia aliongeza Tanzania Daima akisema linamilikiwa na mmoja wa wabunge; akasisitiza kuwa kama ni msumemo ukate kote.Mbunge wa Mlalo, Rashidi Shangazi (CCM) amesema changamoto iliyopo ni hali ya kila Mtanzania kuwa mwanahabari kwa kusambaza chochote kupitia mitandao ya kijamii.Alishauri pia vyombo vya habari viangaliwe ikiwa ni pamoja na kushirikiana na wadau kutengeneza mitaala.Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Mollel (CCM) ambaye alisisitiza kuwa hakuna uhuru usiokuwa na mipaka, alisema Tanzania ni nchi ya pili kwa nchi za Afrika Mashariki kwa uhuru habari. Akihitimisha michango kabla ya bajeti ya wizara yake kupitishwa, Waziri Mwakyembe alisema wabunge 46 wamechangia hotuba yake. Kati yao, 28 walichangia kwa maandishi na 18 kwa kauli.Katika kujibu hoja mbalimbali za wabunge, Dk Mwakyembe alisema habari yoyote inayoandikwa na kuchapisha yenye athari ya kuharibu sifa ya mtu ni kashfa hivyo ni haki kwa mtu aliyekashifiwa kwenda mahakamani kudai fidia kwa maumivu aliyosababishiwa kwa mujibu wa sheria.Akizungumzia adhabu ambazo hutolewa kwa vyombo vinavyokiuka sheria, Mwakyembe alisema, “Tanzania ikitumia sheria ndio utasikia haki za binadamu”.Alisema mwaka juzi yalifungiwa magazeti manne ili wamiliki, waandishi na wadau waelewe kuwa ipo sheria. Mwaka jana hakuna gazeti alilolifungia.Akijibu malalamiko yaliyotolewa na baadhi ya wachangiaji kuhusu gazeti la Tanzanite huku wakinukuu baadhi ya vichwa vya habari vilivyowahi kuchapishwa na gazeti hilo, Dk Mwakyembe alitaja pia kichwa cha gazeti la Tanzania Daima kuwa hakikuwa sawa.“Naomba nisiwadanganye, mimi sikufurahishwa na hicho kitu. Hili ni suala la maadili. Mimi ni mwandishi wa habari naongea naelewa maadili yamekiukwa.“Nimeandika barua ya kumuita anieleze alikuwa ana maana gani? Hilo gazeti (Tanzanite) limetoka tuko kwenye Sikukuu za Pasaka. Tumempelekea barua ameipata na naomba muiamini serikali hatuwezi kufurahia uandishi wa serikali usiofuata maadili.”Awali, Mbunge wa Malindi, Ally Saleh (CUF) alilalamika kuwa licha ya sheria kuwapo, haitekelezwi dhidi ya magazeti yasiyofuata maadili jambo ambalo inawezekana yakakwaza watu wakaamua kuchukua hatua. | 3 |
MBUNGE wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) amesema ni aibu Tanzania kuchukua makocha kutoka nje huku kukiwa na wazawa wenye uwezo mkubwa.Akichangia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa mwaka 2018-2019, Nkamia alisema ni aibu kwa kocha wa mpira wa miguu kutoka Burundi. “Ni aibu kocha wa mpira wa miguu kutoka Burundi huku wazawa wakiwa hawapewi nafasi,” alisema.Nkamia aliyewahi kuwa kiongozi kwenye klabu ya Simba miaka ya nyuma alisema pia kwa sasa Ligi ya Soka ya Wanawake na Ligi Kuu imekuwa mahututi kutokana na timu kulia njaa. “Hata Ligi ya Wanawake hali sio nzuri, mfano timu inatoka nyumbani na ugenini timu inatoka Njombe haina hata sehemu ya kulala kwa sababu ya ukata, hatuwezi kuendesha mpira hivyo.”Kutokana na kauli hiyo, Spika Job Ndugai alisema: “Mheshimiwa Nkamia, sio timu za kina dada tu hata timu fulani zinatembeza bakuli mheshimiwa Nkamia.” Katika hatua nyingine, Mbunge wa Konde Khatibu Said Haji (CUF) amehoji ni kiasi gani cha fedha ambacho kimekuwa kinatolewa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) kwa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA).Akiuliza swali jana bungeni, Haji alihoji: “FIFA inatoa misaada ya fedha kwa kupitia TFF. Je, ni kiasi gani cha fedha TFF imekuwa ikiipatia Zanzibar kupitia ZFA?” Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza alisema ni kweli FIFA inatoa msaada wa fedha kwa mashirikisho ya mpira wa miguu ikiwemo TFF kwa ajili ya miradi na programu mbalimbali.Alisema fedha hizo huwa ni maelekezo maalum kwa lengo la kusaidia na kuendeleza maeneo ya Ligi ya Wanawake, Vijana pamoja na masuala ya kiutawala. “Kuanzia mwaka huu FIFA itakuwa inatoa jumla ya dola za Marekani milioni 1.25 kila mwaka kwa wanachama wake ikiwemo ZFA ambayo ni sehemu ya TFF,”alisema. Akifafanua mchanganuo wa fedha hizo, Shonza alisema fedha za miradi kiasi cha dola za Marekani 750,000, fedha kwa ajili ya kuendesha ofisi dola za Marekani 500,000.“Hata hivyo kwa muda wa miaka mitatu kutokana na kutokuwepo kwa uwazi katika matumizi ya fedha na kukidhi vigezo vya utawala bora, TFF wamekuwa hawapati hizo fedha,” alisema Shonza. Shonza alisema kazi kubwa imefanyika kurekebisha dosari zilizokuwepo za kiuhasibu na utawala bora hivyo uwezekano ni mkubwa TFF na ZFA kuanza kupokea msaada huo wa fedha mapema mwaka huu. | 4 |
Na NORA DAMIAN – DAR ES SALAAM WAKATI mchakato wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwapata wagombea watakaopeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba ukitarajiwa kuanza kesho, joto linaonekana kuanza kupanda. Katika uchaguzi wa mwaka huu, mchuano mkali unatarajiwa kuwa ndani ya chama haswa kwenye nafasi ya Urais wa Zanzibar, ubunge, uwakilishi na udiwani. Ratiba iliyotangazwa juzi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, imegeuzwa kuwa ajenda katika mitandao ya kijamii huku wengi wakihoji iwapo wataibuka wanachama watakaotaka kupambana na Rais Dk. John Magufuli ambaye anatarajiwa kuomba tena ridhaa ya chama chake kuwania ngwe ya pili. Hata hivyo hali hiyo haitarajiwi sana kwasababu CCM ina utaratibu wa kumpitisha rais anayemaliza muhula wake wa kwanza kugombea tena miaka mitano bila kupingwa. Kwa upande wa Zanzibar kumekuwa na mjadala nani atapewa kijiti cha kumrithi Rais wa sasa, Dk. Ali Mohamed Shein, anayemaliza kipindi chake cha pili hasa baada ya kuwapo wanasiasa mbalimbali wanaotajwa kutaka kuwania nafasi hiyo. Katika dakika za lala salama wanaotajwa kugombea wamekuwa wakipigana vikumbo huku baadhi yao wakitumia upepo wa shughuli mbalimbali kujinadi kiaina na wengine wakionekana kufanya harakati za kimya kimya ili kujitengenezea mtaji wa kura katika vikao vya ndani ya chama. Kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM aliliambia MTANZANIA Jumapili kuwa, “huku Bara hakuna shida kazi imeshaisha, gumzo liko Zanzibar subirini.” Rekodi zinaonyesha mbali ya Dk. Shein marais wengine waliowahi kuiongoza Zanzibar ni Sheikh Abeid Amani Karume (1964-1972), Sheikh Mwinyi Aboud Jumbe (1972-1984), Ali Hassani Mwinyi (1984-1985), Idris Abdul Wakili (1985-1990), Salmin Amour (1990-2000) na Amani Abeid Karume (2000-2010). Rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani Karume, alipata wadhifa huo baada ya kutokea mapinduzi yaliyosababisha kupinduliwa kwa Sultani wa mwisho wa Sultan Jamshid bin Abdullah Januari 1964. Miezi mitatu baadaye, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilianzishwa na Karume akawa makamu wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku Mwalimu Julius Nyerere akiwa Rais. Jina la Karume lilirejea tena baada ya Amani Abeid (mtoto wa Karume) kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na kuingia madarakani Novemba 2000 hadi Novemba 2010. WANAOTAJWA ZANZIBAR Miongoni mwa wanaotajwa kuwania urais Zanzibar ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, Balozi Ali Karume, Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni na Waziri wa Viwanda upande wa Zanzibar, Balozi Amina Ali ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 alijitokeza kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea urais wa Jumuhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika orodha hiyo yumo pia aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Zanzibar, Dk. Khalid Salum Mohamed, ambaye aliondolewa kwenye wadhifa huo Machi 3 mwaka huu baada ya kile kilichoelezwa kukaidi agizo la chama chake la kutoanza kampeni kabla ya wakati. Mbali na hao, pia wanatajwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Abood, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Issa Haji Ussi Gavu na Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Hata hivyo Agosti 26, mwaka huu, Samia alisema hana nia ya kuwania urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. urais Zanzibar. UBUNGE, UDIWANI UWAKILISHI Kulingana na ratiba iliyotolewa juzi wanaotaka kugombea ubunge, uwakilishi, udiwani na viti maalumu watachukua na kurejesha fomu Julai 14 hadi 17 mwaka huu. Wanachofanya makada wengi hivi sasa hasa wale wanaotajwa kutaka kugombea nafasi hizo ni kutafuta ushawishi au ‘kiki’ ya kuwafanya waonekane ili kujitengenezea mtaji wakati wa vikao vya ndani na nje ya CCM. Wengine wamekuwa wakiitumia kwa kasi mitandao ya kijamii kujipambanua kwa kueleza yale waliyotekeleza wakati wakiomba kura mwaka 2015. Wamo pia baadhi ya wabunge wa kuteuliwa na wale wa Viti Maalumu ambao pia ni mawaziri wameonyesha dalili ya kutaka kugombea majimbo mbalimbali. Mapema wiki hii wakati akihitimisha hotuba ya Makadirio ya Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2020/21, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, ambaye ni mbunge wa kuteuliwa alisema; “Watanzania msisahau kumpatia rais wetu wabunge na madiwani wanaomudu maadili na mwendo wa Hapa Kazi Tu…na kama itawapendeza wananchi wenzangu wa Buhingwe na chama chetu (CCM) basi iwe pamoja na mimi mtumishi wenu. Jimbo la Buhingwe kwa sasa linaongozwa na Albert Obama. Katika kile kinachoonekana ni kumjibu Dk Mpango, Obama, wakati akichangia bajeti hiyo alisema wananchi wa Buhingwe wanajua alipowatoa na atakapowapeleka na ana imani atapitishwa tena na CCM kugombea jimbo hilo. “Ukija kwenye orodha ya majina yangu bungeni utaambiwa Obama anaitwa nani, utaambiwa ni mashine ya jimbo, mashine ya kusaga na kukoboa, jina la nne utakaloambiwa kwangu ni simba wa yuda la mwisho ni katapila. “Naomba hayo majina yawe katika ‘hansard’ ya Bunge, Buhingwe wanajua tulikotoka, tuliko na tunakoelekea. Niseme 2020 Magufuli hapa, Obama hapa,” alisema Obama. Wachambuzi wa kisiasa wanasema uamuzi wa baadhi ya wabunge wa kuteuliwa na wale wa viti maalumu kuamua kuingia ‘mzima mzima’ katika kinyang’anyiro hicho unachochewa pia na rekodi zao za kiutendaji. RATIBA ILIVYO Kwa mujibu wa Polepole, kwa upande wa Tanzania Bara tukio la kwanza litakuwa ni uchukuaji fomu kwa nafasi ya kiti cha urais, litakaloanza Juni 15 hadi 30 mwaka huu. Alisema tukio la pili ambalo litakwenda sambamba na muda huo wa siku 15 ni utafutaji wa wadhamini mikoani. Alisema tukio la tatu litakuwa ni vikao vya uchujaji, ambapo Julai 6 hadi 7 mwaka huu, kitaketi kikao cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kitakachoanzisha mchakato wa uchujaji, kisha Julai 8 mwaka huu kitaketi kikao cha Kamati ya Usalama na Madili ya Taifa chama hicho. “Julai 9 mwaka huu, kitaketi Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, ambacho kitatoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM juu ya majina ya wanachama wasiozidi watano, wanaoomba kugombea nafasi hiyo ya urais,”alisema Polepole. Vilevile Polepole alisema Julai 10 mwaka huu, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kitapendekeza kwa Mkutano Mkuu wa CCM, majina yasiyozidi matatu ya wanachama wa chama hicho, wanaoomba kugombea urais. Katibu huyo wa itikadi na uenezi wa CCM, alisema Julai 11 hadi 12 mwaka huu, Mkutano Mkuu wa CCM Taifa utachagua jina moja la mgombea wa urais wa Tanzania. ZANZIBAR Kwa upande wa Zanzibar, Polepole alisema Juni 15 hadi 30 mwaka huu itakuwa ni tukio la uchukuaji fomu na kurejesha. “Juni 15 hadi 30 mwaka huu, kutafuta wadhamini mikoani, baada ya hapo vitafuata vikao vya uchujaji, Julai 1 hadi 2 mwaka huu, itaketi Sekretarieti ya Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar, Julai 3 kitaketi kikao cha Kamati ya Usalama na Maadili Zanzibar,”alisema Polepole. Polepole alisema Kikao cha Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM kitakuwa Julai 4 mwaka huu kwa ajili ya kutoa mapendekezo juu ya wanachama waliojitokeza kuomba kugombea urais wa Zanzibar. “Kikao hicho kitafuatiwa na Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri ya Taifa kitakachoketi Julai 9 kwa ajili ya kupendekeza majina matatu ya wanachama wanaoomba kugombea kiti hicho. Kisha, Julai 10 mwaka huu, Halmshauri Kuu ya Taifa ya CCM kitachagua jina moja la mgombea. Aidha alisema Julai 11 hadi 12, Mkutano Mkuu wa CCM taifa utaketi kwa ajili ya kuthibitisha jina la mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa | 3 |
WASHINGTON, MAREKANI RAIS wa Marekani, Donald Trump ameamua kuweka saini ya kuondoa baadhi ya marufuku ya kisheria ambayo mitandao ya kijamii inayo. Saini hiyo inampa mamlaka ya kuweka hatua za kisheria dhidi ya kampuni za mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter katika sheria walizoweka katika maudhui wanayochapisha katika mitandao yao. Rais Trump ameishutumu mitandao ya kijamii kwa kushindwa kuwa makini wakati wa kusaini mamlaka ambayo iko huru kuondolewa wakati wa kuweka saini. Amri hiyo inatarajiwa kukabiliwa na changamoto za kisheria. Wataalamu wa kisheria wanasema kuwa bunge la Marekani au mfumo wa mahakama lazima ihusike ili kubadili sheria iliyopo sasa ambayo inaeleweka kuwa inalinda mitandao ya kijamii. Donald Trump ameilaumu Twitter kwa kuingilia uchaguzi wa urais wa Marekani wa 2020 Trump amekuwa akiishutumu mitandao ya kijamii kila mara kuhariri sauti yake au hata kuweka sauti ambayo hajazungumza lakini anakuwa anasikika kama yeye. Jumatano, Trump aliishutumu Twitter kwa kuingilia uchaguzi baada ya kuongeza maelezo ya tweet mbili kama uthibitisho. Alhamisi , Twitter iliongeza taarifa za kuhakiki taarifa kuhusu Covid-19” na kujumuisha ujumbe wa tweet kutoka kwa msemaji wa serikali ya China anayedai kuwa virusi vya corona vilitengenezwa Marekani. Amri hiyo inasemaje? Amri hiyo imewekwa ili kufafanua sheria ya mawasiliano ya staha ambayo Marekani imeweka katika mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter na Youtube pamoja na ulinzi wa kisheria katika hali fulani. Chini ya kifungu cha sheria cha namba 230, mitandao ya kijamii haiwajibishwi kwa maudhui ambayo watumiaji wake wanaweka mtandaoni lakini inaweza kuhusika kwa upande wa usamaria mwema wa kuondoa maudhui hayo mtandaoni ambayo labda yana maudhui ya unyanyasaji, chuki na yanaaibisha . Amri hiyo maalumu inaainisha kuwa sheria ambayo italinda maudhui ya mitandao ya kijamii kama maudhui hayo hayajabilishwa kwa kuhaririwa na mtumiaji wa mtandao huo na kutaka sheria hiyo ibadilishwe au kuondolewa na wabunge kwa kifungu namba 230. Trump alisema Mwanasheria Mkuu, William Barr ataanza mara moja kuandaa sheria ambayo itapigiwa kura. | 2 |
MVUA iliyonyesha kwa vipindi tofauti juzi na jana katika maeneo mbali mbali ya Jiji la Dar es Salaam, imekatisha kwa muda mawasiliano katika baadhi ya maeneo ikiwamo Barabara ya Morogoro hususani eneo la Jangwani.Hali hiyo imesababisha magari yanayotumia barabara hiyo, kutumia barabara mbadala ili kuendelea na safari. Mvua hiyo iliyonyesha kuanzia juzi jioni hadi jana mchana, kwa kiasi kikubwa ilisababisha eneo hilo la Jangwani, kufurika maji yaliyokuwa yakipita juu ya daraja sambamba na maeneo mengine ya barabara hiyo na hivyo kusababisha magari yakiwemo mabasi ya mwendokasi kushindwa kupita.Aidha, katika hatua nyingine Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema uwepo wa mvua hizo zinazonyesha mfululizo katika baadhi ya maeneo ya Pwani ya Kaskazini ikihusisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, zimesababishwa na kuimarika kwa ukanda wa mvua (ITCZ). Kwa mujibu wa Meneja wa Kituo Kikuu cha Utabiri kutoka TMA, Samweli Mbuya, mvua hizo zinatarajiwa kuendelea hadi kesho na baadaye mvua kama hizo kujirudia tena katikati ya mwezi huu.“Athari za mvua zilizonyesha katika kipindi cha wiki moja mfulululizo katika ukanda wa pwani ya Kaskazini pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba zimesababisha kutuama kwa maji na mafuriko, hivyo kutokana na ardhi kuwa na unyevunyevu mwingi, ongezeko kidogo la mvua linaweza kuendelea kusababisha athari kama zilizokwishajitokeza,” alisema Mbuya.Aliwataka wananchi hao, kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa na kuzingatia tahadhari zilizotolewa na mirejeo yake pamoja na kupata ushauri wa miongozo ya wataalamu katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo. Awali gazeti hili lilitembelea maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam likiwemo Jangwani na kushuhudia maji hayo yakiwa yamefurika katika eneo hilo. | 3 |
MAMLAKA ya Mapato Nchini (TRA) imesema fedha za kodi zinazokusanywa Zanzibar kutoka kwa wananchi na wafanyabiashara zinabakia visiwani kwa ajili ya shughuli za maendeleo.Hayo yalisemwa na Ofisa kodi TRA, Omar Abdalla Kirobo katika mkutano na masheha na madiwani kuwaeleza umuhimu wa kulipa kodi huko visiwani Pemba. Alisema zipo dhana za baadhi ya watu ikiwemo wafanyabiashara kwamba fedha za kodi zinazokusanywa Zanzibar jioni hupelekwa Tanzania Bara kwa matumizi ya huko. “Si kweli fedha za kodi zinazokusanywa Zanzibar zinabakia hapa na kutumika kwa ajili ya shughuli za maendeleo kwa wananchi wa Unguja na Pemba,” alisema.Kirobo alisema kwamba nchi haiwezi kupata maendeleo na kutekeleza miradi ya jamii kama wananchi na wafanyabiashara watashindwa kulipa kodi inayostahiki kwa mujibu wa sheria. Ofisa wa Elimu ya kodi na huduma kutoka TRA, Abdalla Seif aliwataka viongozi wa shehia ikiwemo masheha na madiwani kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari kwa ajili ya maendeleo ya taifa.Baadhi ya madiwani na masheha waliitaka mamlaka kutoa elimu zaidi kuhusu umuhimu wa kulipa kodi ili jamii ifahamu malengo yake na fedha zinazokusanywa zinatumika kwa ajili ya kazi gani. “Tatizo moja kubwa jamii yetu haifahamu umuhimu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa, lakini na taasisi za mapato nazo zitoe elimu zaidi,” alisema Khatib Chwaya, sheha wa Wete Pemba. | 3 |
YOKOHAMA, JAPAN KIUNGO mshambuliaji wa Manchester City, Raheem Sterling amesema alifurahi kuona klabu yake ya zamani ya Liverpool ikishinda taji la Ligi ya Mabingwa msimu uliopita. Liverpool ilitwaa taji hilo, baada ya kuichapa Tottenham Spurs bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa Uwanja wa Wanda Metropolitano Madrid, Hispania . Hata hivyo, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, alisema kuwa Manchester City kushinda taji la Ligi Kuu England ilikuwa muhimu zaidi. Sterling aliondoka Merseyside mwaka 2015 na kujiunga na Man City katika hali ambayo iliwachefua mashabiki wa Liverpool kutokana na nyota huyo kulazimisha kuondoka katika kikosi chao, akiwa mchezaji muhimu. “Nilifurahishwa sana na wao kushinda taji hilo, nimefurahi baadhi ya wachezaji ambao kuchukua ubingwa Ligi ya Mabingwa, ni jambo kubwa kwetu, lakini jambo letu muhimu zaidi ni kushinda Ligi Kuu hilo ndilo lengo letu kuu kuelekea msimu ujao. “Ndiyo, itakuwa vizuri kushinda Ligi ya Mabingwa lakini kwanza tunataka kushinda ligi.Ligi Kuu ni mkate na siagi yako, kila wikiendi unajifunza kitu kipya , Ligi ya Mabingwa ndiyo inayoonekana vizuri na ya kifahari kama watu wanavyosema, lakini kila mwishoni mwa wiki unahama kwenda kukutana na mazingira magumu,”alisema Sterling. City ilishinda taji la Ligi Kuu Eng;and katika dakika za mwisho msimu uliopita, ikimaliza msimu ikiwa na pointi 98, ikifuatiwa kwa karibu na Liverpool iliyomaliza na pointi 97. | 4 |
Mwanamuziki wa Rumba kutoka Congo DRC, Koffie Olomide ambaye amekuja hapa nchini kwa ajili ya shoo amesema Nandy ni miongoni mwa wasanii wa bongo wanaomkosha. Pamoja na Nandy Koffie amesema huwa anaufutilia mziki wa Tanzani na anamfahamu Diamond Platinumz. Katika mahojiano yake ya Clouds Fm Koffie amesema anavutia na wimbo wa kivuruge wa Nandy na amesema amepanga kuingia studio na msanii huyo. “Nampenda sana Nandy na wimbo wake wa Kivuruge ambapo kila nikiusililza nasikia raha, kama mnayo niwekeni,” amesema Koffie. Pia amebainisha kuwa leo ndiyo mara ya kwanza amekutana nanaye na tayari wameongea mipango ya kufanya naye kazi ambapo karibuni wataingia studio.
studio. Jahazini leo The Big Boss himself @josephkusaga akamuuliza @koffiolomide_officiel ni wasanii gani ambao anawafauatilia na kuwakubali kipande hiki cha +255, na majibu ya Mopao yalikuwa "Leo nilikutana na msanii anaitwa @officialnandy, sikuwa namfahamu kabla ila wimbo wake wa Kivuruge nimeupenda sana" Mopao hakuishia hapo ikabidi aombe apigiwe kKvuruge na kilichotokea baada ya kupigiwa ni kuipitia kwa juu kama uonavyo kwenye Video. Unahisi kuna lolote ambalo @officialnandy inabidi ajiongeze kwa Mopai!? A post shared by Clouds FM🇹🇿 (@cloudsfmtz) on Mar 6, 2020 at 9:37am PST | 1 |
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM BENKI ya I&M Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, lakini inang’ara kwa kutoa bidhaa na huduma za kipekee ambazo zinakidhi mahitaji yote ya mteja katika soko. I&M Tanzania ilitambulisha akaunti mpya ya wanawake ya Tunaweza inayotoa suluhisho kwa wanawake wa ngazi zote kuanzia mmoja mmoja, wajasiriamali hadi kikundi au taasisi. Akaunti hiyo inajitofautisha kwa kutoa huduma bila malipo yoyote, haina makato ya kila mwezi na viwango vyake vya riba vinavutia kwenye akiba. Akizungumza leo jijini Dar es Salaa, katika maonyesho hayo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo, alisema kuwa bidhaa hiyo mpya imeunganishwa kwenye mtandao wa benki wa kidijitali ili kuwapa wateja huduma bora na endelevu wakati wowote wanapohitaji. Alisema I&M Tanzania ni sehemu ya I&M Holdings Kenya iliyoanzishwa mwaka 1974 kama kampuni ya huduma za kifedha kabla baadaye kubadilishwa kuwa benki ya biashara. “Mwaka huu inasherehekea miaka kumi ya huduma zetu katika soko la Tanzania. Tunafurahi kuendelea kuhudumia wateja wetu na wateja wapya, pia tunashukuru wateja wetu na washikadau wote walioshiriki katikakuiletea benki mafanikio makubwa kwa kipindi chote cha miaka kumi kwenye soko.” “Tunatoa huduma kadhaa za kifedha ikiwa ni pamoja na akaunti ya akiba, current akaunti kwa madhumuni ya biashara, mikopo ya biashara, huduma za kubadili fedha, uhamishaji fedha kitaifa na kimataifa, huduma za kidijitali ambazo hutoa fursa kwa mteja kupata huduma za benki kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *150*32# au kupitia iClick- huduma ya benki kwa njia ya mtandao inayopatikana bila kikomo kwa saa 24,” alisema Anitha Meneja Masoko na Mawasiliano huyo wa benki hiyo, alisema kuwa pia benki yao wanatoa unafuu na urahisi wa kupata mikopo na huduma nyingine kadhaa ambazo ziliwafanya watu waliotembelea banda lake kwenye maonyesho ya Sabasaba lililopo ukumbi wa Karume, upande wa kulia wa lango la kuingilia kuhamasika na kutaka kujua zaidi kuhusu benki hiyo. “I&M inafungua milango kwa Watanzania wote kwenda kujiunga na benki inayojali mahitaji yao, iliyo tayari kuwapa huduma za kipekee za kifedha kupitia wafanyakazi wake wenye uzoefu zaidi katika kutoa huduma bora kwa wateja. “Mbali na kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba, benki hiyo inatoa huduma zake bora kupitia mtandao wa matawi yake yaliyoko maeneo ya Maktaba, Indira Gandhi, Nyerere, Kariakoo, Oysterbay pamoja na mikoani ikiwa ni pamoja na Moshi, Arusha na Mwanza,” alisema Timu ya wafanyakazi wa mauzo na idara ya masoko wa benki hiyo kutoka matawi yake ya Dar es Salaam inayoongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wapo kwenye maonyesho hayo ili kuwapa wageni na wale ambao wanataka kuwekeza katika benki inayoaminika na salama ikiwa na huduma za ATM zinazopatikana kwa saa 24. | 5 |
WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia leo inatarajia kuwatunuku wanafunzi 29 waliofanya vizuri matokeo ya mitihani ya taifa mwaka 2018.Aidha, shule 40 ambazo zimetoa wanafunzi bora zaidi pia zitazawadiwa wakati wa kilele cha Wiki ya Elimu ikiwa ni kutambua jitihada zao katika maendeleo ya sekta ya elimu.Hayo yalielezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa wizara hiyo, Sylvia Lupembe.Amesema wanafunzi bora 29 kwenye matokeo ya mitihani ya taifa kwa mwaka 2018 yaliyotolewa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) kwa mitihani ya shule za msingi, kidato cha nne na kidato cha sita watazawadiwa.Lupembe alisema kati ya wanafunzi wanaopewa tuzo zao leo, 10 ni wa shule za msingi, 10 kwa kidato cha nne na tisa kutoka kidato cha sita.Alisema Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako ndiye atakuwa mgeni rasmi wa utoaji wa tuzo hizo.Alisema hafla hiyo itafanyika katika Shule ya Sekondari ya Msalato nje kidogo ya Dodoma.Aliomba wadau wa elimu kujitokeza kwa wingi katika tukio hilo ili kuwapongeza wanafunzi na shule zilizofanya vizuri katika mitihani yao.Lipembe aliwataja wadau watakaohudhuria ni maofisa wa elimu na waratibu wa elimu wa kikanda, washirika wa maendeleo na uongozi wa kikanda na mamlaka za serikali za mitaa.Alisema wizara itaendelea na kazi ya kutambua juhudi zilizofanywa na wanafunzi na shule katika kuboresha ubora wa elimu kila mwaka. | 3 |
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wananchi kwenye Kata ya Mnacho wilayani Ruangwa washirikiane kujenga mabweni katika Shule ya Sekondari Mnacho ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu kwenda shuleni hapo.Aliyasema hayo wakati alipotembelea shule hiyo kwa ajili ya kukagua mradi wa ujenzi wa bweni, ambalo ujenzi wake unagharimu Sh milioni 92.4 ikiwa ni mchango uliotolewa na wadau wa elimu.“Bweni hili likikamilika litawapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kuja shuleni hususani wanaoishi vijiji vya mbali kwa sababu wataishi hapa, jambo ambalo litachangia kuongeza ufaulu wa watoto wetu.”Kadhalika, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi waishio katika kata hiyo na za jirani washirikiane na kuanzisha mradi wa ujenzi wa mabweni mengine kwa kuwa hilo moja lililojengwa na wadau halitoshi kulingana na idadi ya wanafunzi.Alisema yeye yuko tayari kuendelea kuwaunga mkono wananchi hao kwenye mipango yao yote ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata yao, lengo likiwa ni kuhakikisha mikakati ya serikali ya kuboresha huduma za jamii inatimia.Hata hivyo, Waziri Mkuu aliwataka wananchi hao washirikiane na walimu kufuatilia maendeleo ya taaluma kwa watoto wao shuleni na kujiridhisha kama wanafanya vizuri darasani na iwapo watabaini changamoto waweze kuzitatua kwa pamoja.Akisoma taarifa ya ujenzi wa bweni hilo, Mkuu wa Shule ya Sekondari Mnacho, Mwalimu David Mwakalobo alisema ujenzi wa bweni hilo lenye uwezo kulaza wanafunzi 80 ulianza Septemba 19, mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Januari, 2019. | 3 |
PYONGYANG, KOREA KASKAZINI KOREA Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kulifanyia jaribio bomu la nyuklia, ambalo linaweza kuwekwa kwenye kombora la masafa marefu. Taifa hilo la kikomunisti lilisema jaribio hilo la sita la bomu la nyuklia, lilifanikiwa saa kadhaa baada ya mitetemeko mitatu kutambuliwa. Ilidai kulifanyia jaribio bomu la haidrojeni, ambalo lina nguvu zaidi kuliko bomu la nyuklia. Wadadisi wanasema kuna ishara kuwa uwezo wa nyuklia wa Korea Kaskazini unazidi kukua. Watabiri wa hali ya hewa mapema walitambua uwapo wa tetemeko dogo la ardhi, eneo ambalo Korea Kaskazini ilikuwa ikifanyia majaribio ya nyuklia. Tetemeko hilo lilitokea saa kadhaa baada ya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un kupigwa picha akiwa na kile ambacho vyombo vya habari vilisema kuwa aina mpya ya bomu la hydrogen. Vyombo vya habari vilisema kuwa kifaa hicho kinaweza kutundikwa kwenye kombora la masafa marefu. Muda mfupi baadaye Rais wa Korea Kaskazini, Moon Jae-in aliitisha mkutano wa dharura wa baraza za lake la usalama wa taifa. Ripoti za awali kutoka kwa Idara ya Hali ya Hewa ya Marekani zilitaja tetemeko hilo kuwa la ukubwa wa kipimo cha 5.6 Richter, lakini baadaye likasema kuwa ukubwa huo ni 6.3 Richter. | 2 |
WAKUU wa nchi mbalimbali Afrika wamesema bara hilo limepoteza shujaa mkubwa wa harakati za ukombozi wa bara hilo, Robert Mugabe (pichani) na kutaka uzalendo na umoja wake uendelee kuenziwa huku Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa akitumia muda huo kuomba radhi kwa vurugu walizofanyiwa wageni Waafrika nchini mwake.Aidha, Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa amesema nchi hiyo imefunga rasmi suala la mgogoro wa ardhi akisema kamwe nchi hiyo haitafanya marekebisho ya sheria ya ardhi, na ardhi iliyopo ni ya Wazimbabwe na itatumika kwa ajili ya maendeleo yao na sio vinginevyo. Viongozi hao wametoa kauli hizo jana kwenye Uwanja wa Mpira cha Rufaro jijini Harare kwenye shughuli ya mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Zimbabwe, Komredi Mugabe, na kutoa heshima zao kwa mwili wake. Zaidi ya marais wa sasa 10 walishiriki wakiwamo pia marais wastaafu wa Afrika na wawakilishi kutoka mataifa mbalimbali ambao walimzungumzia Mugabe kama kiongozi shujaa na mwanamapinduzi wa kweli wa Afrika. Baadhi ya marais hao ni Uhuru Kenyatta wa Kenya, Edgar Lungu wa Zambia, Filipe Nyusi wa Msumbiji, Dk Hage Geingob wa Namibia, Teodoro Nguema wa Equatorial Guinea, Ramaphosa, Andy Rajoelina wa Madagascar, Peter Mutharika wa Malawi, Joao Laurenco wa Angola na Brahim Ghali wa Jamhuri ya Kiarabu ya Sarhawi.Akitoa salamu za rambirambi, Rais Ramaphosa alilazimika kuomba radhi kutokana na mauaji na vurugu wanazofanyiwa Waafrika nchini humo, baada ya kuanza kuzomewa aliposimama kutoa salamu zake.“Niombe radhi kwa kilichotokea Afrika Kusini dhidi ya Waafrika wenzetu, ni kweli kilichofanyika kimekwenda kinyume na makubaliano ya Umoja wa Afrika ambao waasisi wake akiwemo marehemu Mugabe alisisitiza tuwe kitu kimoja na tushikamane,” alisema Rais Ramaphosa.Aliongeza, “Tukio lile ni baya na hata nyie mmelisema hapa kwa ujumbe wenu na mimi niko nakubaliana na nyie, tunalifanyia kazi kuhakikisha jambo hilo halitokei, sisi sio wabaguzi tunapenda wageni na tunaalika watu mbalimbali kuja kuwekeza hii ndio njia ya kumuenzi Mugabe kiongozi wetu shujaa.”Naye Rais Uhuru Kenyatta akimzungumzia Mugabe, alisema Afrika imepoteza kiongozi aliyekuwa alama ya ukombozi na mwenye uzalendo na nchi yake lakini pia kwa bara zima.“Tumempoteza alama ya kweli ya ukombozi wa bara letu, Mugabe alikuwa mstari wa mbele kusema matatizo ya Afrika na alipigania kupatikana kwa suluhu yake, kilichobaki ni sisi viongozi wa sasa kumuenzi mema yake kwa kuungana kuweka maslahi ya wananchi wetu na bara letu, hii ndio nje pekee ya kumuenzi,” alisema Uhuru. Akizungumzia kifo cha Mugabe na suala la ardhi, Rais Mnangagwa alisema mti mkubwa wa Afrika umedondoka na bara zima liko kwenye majonzi na ili kumuenzi shujaa huyo, Zimbabwe itaendelea kuheshimu mabadiliko ya matumizi ya ardhi yaliyofanywa na Mugabe na kamwe nchi hiyo haitafanya marekebisho ya sheria ya ardhi.“Zimbabwe kamwe haitafanya marekebisho ya sheria ya ardhi , ardhi yote ni ya Wazimbabwe na sio vinginevyo, na katika kumuenzi baba yetu Mugabe tutaheshimu maamuzi aliyoyafanya kuhusu umiliki wa ardhi na kamwe hatutabadilika,” alisisitiza Rais Mnangagwa aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Mugabe.Aidha, aliitaka jumuiya ya kimataifa kuondoa vikwazo vya kiuchumi nchi hiyo kwani imeshasema wazi ardhi yake itatumika kwa maendeleo, na wameshachukua hatua kadhaa kufanya mapinduzi ya kiuchumi. Pia aliishukuru Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Afrika (AU) kwa kuwa mstari wa mbele kusimama nao na kutaka vikwazo dhidi yao viondolewe.Akimzungumzia Mugabe, alisema Bara la Afrika lilikuwa limebakiwa na waasisi wawili wa ukombozi ambao ni Mugabe na Rais wa zamani wa Zambia, Kenneth Kaunda na sasa Mugabe ameondoka na amebaki mmoja.“Kwa kweli tunasikitika kuondokewa na kiongozi wa ukombozi wa bara letu walikuwa wamebaki wawili yeye na Kaunda sasa Kaunda kabaki mwenyewe, Mugabe kaenda kuungana na waliom tangulia kama akina hayati Mwalimu Julius Nyerere, Nelson Mandela na wengine wale waasisi wa ukombozi wa Afrika,” alisema Mnangagwa.Naye Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan aliyemwakilisha Rais John Magufuli, alisema Tanzania inalia pamoja na Wazimbabwe, na msiba huo ni wa bara lote na Mugabe alifanya mengi yaliyoacha alama. “Tanzania iko na nyie, tunalia pamoja marehemu Mugabe atakumbukwa daima kwa mema aliyofanya kwa nchi yake, lakini pia kwa Bara la Afrika, alikuwa kiongozi mwenye utu na uzalendo wa kweli,” alisema Samia.Kwa upande wake, Rais Nguema alisema Mugabe alikuwa mpigania haki za binadamu na mwanaharakati wa kweli wa ukombozi hivyo mchango wake kamwe hautasahaulika. Wakati Rais Jamhuri ya Kiarabu ya Sahrawi, Brahim Ghali alisema Mugabe atakumbukwa kwa mchango wake wa ukombozi wa Afrika alisema alikuwa kiongozi shujaa wa uhuru na mwenye utu wa kweli.“Mugabe alikuwa kiongozi mwenye utu,alichukua jambo kama lake na hata sisi watu Sahrawi ametusaidia sana kwenye mgogoro wa mipaka, daima tutamkum buka,” alisema Ghali.Naye Mwakilishi wa Cuba, Casa Ines- Maria alisema Mugabe alikuwa kiongozi mzuri mwenye kujenga uhusiano bora na mataifa mengine rafiki na kwamba uhusiano wake na marehemu Fidel Castro ulianza zamani na kwamba hadi leo unaendeleo baina ya nchi hizo.Mwakilishi wa China, Hou Xi Jou alisema Rais Xi Jinping ametuma salamu za rambirambi na kusema Mugabe alitoa mchango mkubwa katika kuhimiza urafiki kati ya China na Zimbabwe na kati ya China na Afrika.Marais wastaafu wa Afrika waliohudhuria ni Kaunda, Jerry Rawlings wa Ghana, Thabo Mbeki na Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Joseph Kabila wa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Olusegun Obasanjo wa Nigeria.Mugabe (95) aliyeitawala Zimbabwe kwa miaka 37 kati ya 1980 hadi 2017 alipoondolewa madarakani kwa msaada wa jeshi, alifariki dunia wiki iliyopita nchini Singapore alikokwenda akipatiwa matibabu.Serikali ya Zimbabwe na familia yake imesema maziko yake yatafanyika kwenye Makaburi ya Mashujaa katika Kiwanja cha Mashujaa wa Taifa. Aidha, tarehe rasmi ya maziko haijafahamika na sherehe za kimila za kumuaga zitafanyika kijijini kwake na hiyo ni kwa mujibu wa taafira za familia. | 3 |
Picha za harusi ya mapacha hao watatu wa kiume na wa kike. Picha: Hisani Mapacha hao waliandaa sherehe ya harusi katika jimbo la Enugu Nigeria Sherehe hiyo ya faragha ilhudhuriwa na waalikwa pekee Picha za harusi ya mapacha hao watatu wa kiume na wa kike zimeibua mjadala mkubwa mitandaoni Mitandao ya kijimaa iliwaka kwa ucheshi mkubwa huku picha za harusi za mapacha watatu wa kiume na kike zikisambaa kote. Picha za mapacha hao wa kike wanaofanana kama shilingi kwa ya pili, Okwoma, Dumalu na Chinwe ziliwaacha wengi vinywa wazi haswa baada ya kubainika kuwa waliolewa na mapacha wengine watatu. The Triplets walked down the aisle in grand style.Congratulations 🎤 to them…😍😍😍😍😍Chinedu Weds Dumalu, Chukwuebuka… Posted by Diva Anita Brown on Sunday, 7 June 2020 Picha zao zilichapishwa katika mtandao wa facebook na mwanadada aliyetambulika kama Diva Anita Brown aliyekuchukua nafasi ya kipekee kuwapa heko kwa hatua walioichukua. ‘’ Mapacha hawa walifunga pingu za maisha kwa njia ya aina yake. Heko kwao. Chinedu amuoa Dumalu, Chukwuebuka amuoa Okwuoma na Kenechukwu amuoa Chinwe. Tunasherehekea harusi ya mapacha hawa, pia ilete baraka kwetu sote.’’ Anita aliandika. Sherehe ya harusi ya mapacha hao iliandaliwa faraghani, waalikwa pekee wakiruhusiwa kuhudhuria. Mitandao iliwaka huku wengi wakiwarashia kwa jumbe za heri na pongezi na kuwatakia mema katika ndoa yao. Kilichosalia kuwa swali kwa wengi ni kuhusu jinsi sita hao walivyokutana pamoja, wakapendana na kupanga kuoana. Kweli hakuna kisichowezekana. Hapa Bongo Leo, tunawataki kilalaheri na baraka za ndoa. | 1 |
Na JANETH MUSHI-ARUSHA WABUNGE wa Chadema, Godbless Lema (Arusha Mjini) na Joshua Nassari (Arumeru Mashariki),wanatarajia kuwasilisha ushahidi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola kuhusu madiwani wa chama hicho waliojiuzulu kutuhumiwa kupokea rushwa. Hatua hiyo, inakuja zikiwa zimepita siku tano tangu wabunge hao walipodai madiwani hao walihama kuunga mkono rushwa na si kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli kama walivyodai. Lema jana aliliambia MTANZANIA kuwa tayari wamezungumza na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe ambapo alitoa maelekezo kwao kupeleka ushahidi huo Takukuru. “Nassari anakuja kesho kutwa (kesho), kutoka Nairobi, amezungumza na Mbowe ambapo alitoa maelekezo, hivyo Nassari akija nchini tutapanga kwenda kumwona Mkurugenzi wa Takukuru,” alisema Lema. Jumapili wiki hii, Nassari aliwaambia waandishi wa habari kuwa anaoushahidi usiokuwa na shaka kuhusu madiwani wa Chadema waliohamia CCM kuhongwa. Kutokana na hilo, Nassari alisema endapo ushahidi huo hautakuwa wa kweli atajiuzulu ubunge wake. Pia alisema yupo tayari kukutana kukutana na Rais, Mkurugenzi wa Takukuru, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai(DCI),Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa,kuwaonyesha ushahidi usiotia shaka na kwamba baada ya siku 14 asipoitwa kuonyesha ushahidi huo atauweka hadharani. Hadi sasa madiwani tisa wa Chadema wamejiuzulu na kuhamia CCM ambapo kati ya hao, watano wanatoka Jimbo la Arumeru Mashariki,Arusha Mjini wawili,Monduli mmoja na Longido mmoja. | 3 |
Na JENNIFER ULLEMBO-DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya wanawake wenye umri chini ya miaka 20 ‘Tanzanite’, Sebastian Nkoma, amesema kuwa anatarajia kikosi chake kitapunguza idadi ya mabao ya kufungwa kwenye mchezo wa marudiano dhidi ya Nigeria, Jumapili Uwanja wa Uhuru. Akizungumza na MTANZANIA jana, Nkoma alisema kikosi chake kilipata kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Nigeria katika mchezo wa awali kutokana na ugeni wa mashindano ya kimataifa. Alisema hivi sasa timu yake imefanikiwa kufanyia kazi makosa yote yaliyojitokeza kwenye mchezo wa kwanza, hivyo matumaini yake ni kupunguza idadi ya mabao waliyofungwa na Nigeria. “Tumejipanga katika mchezo wa marudiano tupunguze idadi ya mabao ya kufungwa au tushinde, kule Nigeria wenzetu wana uzoefu wa muda mrefu sana tofauti na sisi,” alisema. “Mpira ni mchezo wa makosa, unapokosea unajifunza, hivyo nikiwa kama mwalimu nimejitahidi kwa uwezo wangu kukijenga kikosi changu na kuwaondoa hofu wachezaji,” alisema Nkoma. Nkoma alisema Nigeria wana kikosi kizuri, ambacho kimeandaliwa kwa muda mrefu na kucheza mechi mbalimbali za kimataifa tofauti na Tanzania. Mara baada ya kurejea, kocha mkuu wa timu hiyo, Nkoma, amesema walipoteza mchezo wa awali kwa kufungwa mabao 3-0 kwa sababu Nigeria ni timu bora na Tanzanite kwa sasa wanajipanga kwa ajili ya mchezo wa marudiano. | 4 |
MWENYEKITI wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Leodogar Tenga amemtaka Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallence Karia kuacha kuliongoza shirikisho hilo kirafiki.Tenga amesema hayo mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF uliofanyika Jijini Arusha na kuhudhuriwa na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.Amesema hakuna mtu asiyekuwa na rafiki, lakini urafiki una mipaka na ukiweka urafiki mbele katika majukumu ya kazi ya kila siku ya shirikisho hilo, basi unaweza kukwama mbele na kuanza kulaumiwa.Mwenyekiti huyo alimtaka Rais wa TFF kuacha urafiki katika kuliongoza shirikisho hilo na badala yake alimtaka kuongoza kwa kufuata misingi ya Katiba ya TFF.‘’Kila mtu ana rafiki hapa tulipo na kamwe usiruhusu urafiki uingilie kazi yako ya kuliongoza shirikisho hilo lenye katiba na kanuni katika kuongoza,’’ alisema Tenga, ambaye aliwahi kuwa Rais wa TFF.Tenga alimsifu Gambo kwa kushirikiana na TFF katika kuongoza soka la nchi hii na kusema kuwa hajawahi kuona kiongozi wa mkoa mwenye moyo kama mkuu huyo wa mkoa. | 4 |
NA GEORGE KAYALA BAADA ya kupatikana washindi wa Miss Albino Kanda ya Mashariki na Kaskazini, kwa sasa shindano hilo linatarajiwa kufanyika Kanda ya Ziwa mwishoni mwa mwezi ujao jijini Mwanza ikiwa ni harakati za kuendelea kumsaka Miss Albino Tanzania 2016. Mratibu wa shindano hilo, Alexander Matowo, aliliambia MTANZANIA jana kuwa maandalizi kwa ajili ya kumpata mshindi huyo yanaendelea ambapo tarehe na ukumbi vitawekwa wazi mwishoni mwa wiki hii. Washindi waliopatikana hadi sasa ni Priscilla Samweli wa Kanda ya Mashariki mkazi wa Chanika jijini Dar es Salaam na Eveline Felixoiso wa Kanda ya Kaskazini mkazi wa Boma mkoani Arusha. “Shirika lisilo la kiserikali la Save Vulnerable Foundation (SVF) ndilo linaendesha shindano hilo na lengo ni kutambua thamani ya watu wenye ulemavu wa ngozi ambao wamekuwa wakiuawa kikatili na watu wenye imani potofu na muda mrefu wamekuwa wakitengwa katika jamii hasa kwenye mashindano ya kuwasaka warembo wa Tanzania, hivyo tumeona nao tuwaandalie shindano lao,” alisema Matowo. | 1 |
NA AYOUB HINJO KARIBUNI sana Kariakoo, Wabrazil. Karibuni Dar es Salaam kwa Mheshimiwa Paul Makonda, karibuni sana katika jiji la maajabu. Ni ardhi hii aliyozikwa Steven Kanumba na filamu zake, ni sehemu hii hii anapoteketea Chid Benz na umwamba wake, nini zaidi mnahitaji kujuzwa kuhusu Dar es Salaam? Kila mtu ana sura yake na moyo wake hapa, msidanganyike na vicheko vyao. Wabaya na wazuri wote wapo. Unataka starehe? Zipo hapa, mpaka zile zisizompendeza shetani. Hii ndiyo Dar es Salaam tamu iliyomkimbiza Mr Nice na kumfedhehesha 20 Percent akiwa na utamu wake. Hili ndilo jiji pekee duniani wanakopatikana watu aina ya Shilole, Snura, Amber Lulu, Amber Rutty na Giggy Money kwa wakati mmoja. Wako wazuri hapa wa kila rangi na utakutana nao kama walivyokutana nao mahotelini akina Andrey Coutinho na mwenzake Jaja kipindi kile, uamuzi ni wako vijana wenzangu. Karibu sana. Kama mmekuja na akili zenu kama alivyokuja nazo Emmanuel Okwi kipindi kile, bila shaka mna pepo yako ndogo ya kuishi pale Kariakoo. Ila kama mmekuja na mabegi tu kama alivyokuja nayo Malimi Busungu, basi jiandaeni kuishangaa Kariakoo kama alivyoishangaa Danny Sserunkuma kipindi kile, jiji limekosa adabu hili. Nilivyowatazama na niliyoyasikia baada ya utambulisho wenu Simba, hakika nafsi yangu ilijiridhisha kuwa ‘Dar es Salaam imepata watu wao’. Lile jiji la maajabu sasa limepata watu wao wa maajabu! Japo hata mimi ni miongoni mwa Watanzania wanaosubiri kuona kazi yenu itakavyokuwa katika ardhi hii. Wakati huu ambao naumiza halmashauri ya ubongo wangu kuzidi kuwafahamu, ghafla, nilikumbuka jinsi wale wenzenu waliokuja miaka michache iliyopita pale Jangwani, kusema kweli Kariakoo haikuwaacha salama, kama hawakuwaambia basi mimi nimetoa siri hiyo kwenu. Tatizo ambalo lipo mpaka sasa, mmewagawa mashabiki wa Simba. Ndio, kama mlikuwa hamjui basi acha niwaambie tu. Wapo wanaoamini kuwa mmekuja kufanya kazi iliyowaleta Dar es Salaam, kwa maana hiyo imani zao tayari zipo kwenye miguu yenu lakini wengine bado wanashindwa kutoa maamuzi, kila mmoja anatumia mfano wa majirani zao na akina Jaja. Vijana wenzangu hii ndio Dar es Salaam yenye watu wasiotabirika kwa urahisi. Kwa hiki kipindi kifupi ambacho wote tunaisoma namba, msemaji wa klabu yenu Haji Manara amekuwa mtu muhimu zaidi ndani ya Simba kuliko hata bao la kisigino la Clatous Chama lililoipeleka timu hiyo katika makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Ni yeye ambaye amekuwa akipewa lawama pale timu inapofanya vibaya, mnadhani anajali? Walaa! Amekuwa akiishi hivyo, Simba yote ipo katika mdomo wake uliojaa maneno ya karaha kwa wapinzani. Mmekutana na Patrick Aussems. Kocha anayeamini uwezo kabla ya jina, kocha anayetengeneza mfumo utakaofuatwa na wachezaji na si kuwa na mfumo utakaofuata wachezaji. Macho yakishamdanganya Aussems, hana muda tena wa kuliamini sikio, sababu ni rahisi, kuona ni kuamini. Akili zenu zinatakiwa kutulia mara mbili zaidi ya mnavyotulia mkiwa na mpira miguuni mwenu, ni wakati wenu wa kufungua macho na kuchagua njia mnayotaka kupita. Mnataka sifa na makelele ya Kariakoo? Mtazipata. Ziko laki na viroba vya mchele vinamsubiri kama mkiamua kuwa ‘wafalme wa Kariakoo’. Magazeti hayataacha kuandika habari zenu, mkifanya vyema yatasifia, mkiboronga mtashughulikiwa vilevile, msiyaweke sana akilini japo ni changamoto mnayotakiwa kuizoea. Kitu pekee mnachotakiwa kukumbuka kwa sasa, ni kwamba mpo Kariakoo iliyo ndani ya jiji la Dar es Salaam, mengi yasiowezekana kwingine, hufanyika kirahisi sana hapa. Karibuni sana. | 4 |
MABINGWA wa kihistoria Yanga wamewasili Zanzibar jana kuweka kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo wa Ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana utakaochezwa Jumamosi ya wiki hii.Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 12:00 jioni, kisha baadaye watarudiana kati ya Agosti 23 na 25 Botswana. Akizungumza baada ya kuwasili kisiwani huko Kocha Mkuu Mwinyi Zahera alisema anatarajia baada ya siku tano watakuwa tayari kwa mchezo huo.“Tunashukuru Mungu tumefika Zanzibar salama, ni mara yangu ya kwanza kufika huku, tutaendelea na mazoezi baada ya siku tano, kikosi kitakuwa tayari kwa mpambano huo wa kimataifa,”alisema.Kocha huyo hivi karibuni baada ya kumalizika kwa kilele cha wiki ya Wananchi, alisema anahitaji mechi moja ya kirafiki kwa ajili ya kuendelea kutizama kikosi chake baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Kariobang Sharks ya Kenya.Ombi lake limefanyiwa kazi baada ya Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Fredrick Mwakalebela kusema kuwa kutakuwa na mechi mbili za kirafiki ambapo leo watacheza na Mlendege na kesho dhidi ya Malindi.“Maandalizi yanakwenda vizuri kesho (leo) timu itacheza na Mlandege na kesho kutwa dhidi ya Malindi kwa ajili ya kujipima nguvu kabla ya kurudi ijumaa kwa ajili ya mchezo wetu wa kimataifa,”alisema. | 4 |
MAKAMU wa Ris Samia Suluhu Hassan ameahidi viwanja vya kujengea nyumba kwa wachezaji wa timu ya soka ya Taifa ya wanawake, Twiga Stars endapo watafuzu michezo ya Olimpiki 2020, Japan.Twiga Stars ipo kwenye kinyang’anyiro cha kufuzu michuano hiyo, ambapo juzi ilicheza na Congo DR kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam na kutoka sare ya mabao 2-2.Mama Samia aliyasema hayo jana alipozungumza na wachezaji hao Dar es Salaam ambapo aliwapongeza lwa matokeo ya mechi yao na kuwatakia safari njema katika mechi ya marudiano keshokutwa.Twiga ilitarajia kondoka leo Alfajiri kwenda Kinshasa kwa ajili ya mechi hiyo matudiano itakayofanyika keshokutwa. “Wenzetu wanaume (Taifa Stars) walivyoshinda walipewa zawadi, na mimi nawaahidi mkishinda nitamwomba baba (Rais John Magufuli) awape zawadi kama wenzenu,” alisema. “Jana (juzi) ilikuwa nije lakini nilishindwa kutokana na majukumu ila kwa mara ya kwanza. nilikaa kwenye TV nikatizama mechi dakika zote 90 ingawa kuna wakati nilikasirika na kuna wakati nilifurahi” alisema.Mbali na ahadi hiyo Mama Samia alitoa sh 5,000,000 kwa wachezaji na benchi la ufundi kama mchango wake kwa safari. Aidha, Mama Samia ameahidi kuitafutia timu hiyo wafadhili.“Timu zote za taifa zina wadhimini, mimi kama mama yenu nitawatafutia wadhamini na naomba Jumatatu (kesho) viongozi wenu waje ofisini tuone cha kufanya,” alisema | 4 |
MAPUTO, MSUMBIJI RAIS Filipe Nyusi wa Msumbiji amesema kuwa jeshi la vikosi vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo limekabiliana vikali na wanamgambo vamizi baada ya kushambulia mji wa Macomia katika jimbo tajiri kwa gesi Kaskazini mwa nchi hiyo Alhamisi iliyopita. Mji wa Macomia unaopatikana umbali wa kilomita 230 kutoka Pemba makao makuu ya jimbo la Cabo Delgado ni mji muhimu kuwahi kushambuliwa hivi karibuni tangu kuanza mwaka huu kufuatia kushadidi mashambulizi ya wanamgambo hao wanaotajwa kuwa na mfungamano na kundi la kigaidi la Daesh. Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa mapigano makali yalishuhudiwa baada ya kushambuliwa mji huo. Mapigano hayo yalianza mapema Alhamisi iliyopita kufuatia hujuma ya wanamgambo hao vamizi waliohujumu nyumba za raia na miundo mbinu na kusababisha raia kuyakimbia makazi yao. Rais Nyusi alisema kuwa mapigano yaliyoendeshwa na vikosi vya ulinzi na usalama vya nchi yake yalikuwa makubwa na yaliyozaa matunda. Alisema wamepata taarifa kwamba makada wakuu wa wanamgambo hao wameuliwa. AP | 2 |
WINGI wa mechi za viporo za Simba umeonekana kumtesa na kumkatisha tamaa ya ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera.Wakati Yanga ikiwa imeshacheza mechi 30 na kubakiza mechi nane za kufunga msimu, Simba ina mechi 16 zinazoipa nafasi kubwa ya kutetea taji lake. Hiyo ni kutokana na ukweli kuwa mwenendo wa timu hizo uko tofauti kwani Yanga ilionekana kuyumba katika baadhi ya mechi tofauti ya matarajio yao.Akihojiwa kuhusu mbio za ubingwa baada ya kuifunga mabao 2-0 African Lyon juzi, Zahera alisema kutokana na idadi hiyo ya mechi za wapinzani hajui kama itawezekana kuwa bingwa. “Kuna timu ina mechi 16 ambazo ni sawa na kipande cha ligi nzima wakishinda zote wanabeba ubingwa, kwa sababu ni mechi nyingi kitu ambacho naogopa,”alisema.Alisema hajui ni sababu gani ilicheleweshwa kwa timu hiyo kushindwa kucheza mechi hizo zikabaki huku wengine wakiendelea kucheza. Kihesabu,Yanga katika mechi 30 ilizocheza, imeshinda 23, imepata sare nne na kupoteza michezo mitatu ikiongoza kwa pointi 71 na kama ikishinda michezo yote iliyobaki itafikisha pointi 95.Na Simba imecheza michezo 22, imeshinda 18, sare tatu na kupoteza mchezo mmoja ikiwa na pointi 57 na kutokana na kasi yao ikishinda michezo yote itafikisha pointi 105 ambazo mwingine yeyote hawezi kuzifikisha. Suala la ratiba kutokuwa na viporo vingi kwa timu zinazoshiriki michuano ya kimataifa limeonekana kuwashinda bodi ya ligi, kwani hujitokeza karibu kila msimu. | 4 |
Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba ilisema katika ziara yake ofisa huyo ataonana na wadau mbalimbali wa ndani na nje wa benki hiyo. Mramba alisema lengo ni kujadili mikakati itakayowezesha benki hiyo kukua kibiashara na kusaidia kukua uchumi nchini.Taarifa hiyo ilisema Winters aliteuliwa na Bodi ya Standard Chartered PLC duniani kuwa Mtendaji Mkuu Juni 10, mwaka jana baada ya kujiunga na kundi hilo Mei mwaka huo huo.Ilieleza kuwa tangu aliposhika madaraka, Winters amefanyia mabadiliko mikakati ya benki hiyo na kupitisha mipango ya benki hiyo Afrika. Novemba mwaka jana alitangaza mkakati mpya wa benki hiyo kwa lengo la kupatia sura mpya itakayowezesha kushika fursa muhimu.Alitangaza kuwa benki hiyo imewekeza zaidi ya Dola za Marekani bilioni tatu katika miaka mitatu ijayo huku akipitisha kuipa kipaumbele Afrika katika uwekezaji huo.Kiwango hicho ni ongezeko la asilimia 50 kwa uwekezaji wa sasa na haijawahi kuwekeza kwa kiwango hicho huku akieleza kuwa Afrika ni soko kubwa la benki hiyo na sehemu muhimu ya uwekezaji wake. | 5 |
NA EZEKIEL TENDWA
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilbroad Slaa, amezitolea uvivu klabu za Simba na Yanga kusema hazina jipya.
Slaa alitoa kauli hiyo juzi Jumapili kwenye mkutano wa kumpongeza mwenyekiti mpya wa Serikali ya Kibwegere, Edson Nyingi, uliofanyika kwenye viwanja vya Makombe, Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza na umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza katika mkutano huo, Dk. Slaa alisema kwa sababu Simba na Yanga zimeshindwa kufika popote, ni lazima zitafutwe timu mbadala za kuweza kuchukua nafasi zao.
Alisema anasikitishwa na klabu hizo kwani licha ya ukongwe zilionao katika Soka la Tanzania zimeshindwa kuitangaza nchi kimataifa.
“Sina ugomvi na Simba wala Yanga, lakini lazima tukubaliane kuwa zimeshindwa kuitangaza nchi kimataifa na hii ni kutokana na mipango mibovu ya klabu hizi, hivyo ni wakati wa vijana kujipanga kuanzisha timu zenye malengo.
“Angalia Azam, licha ya kwamba ni timu changa iliyoanzishwa miaka ya hivi karibuni, lakini imeonyesha dhamira ya dhati ya kuleta maendeleo ya soka kama tunavyoshuhudia tayari wana uwanja wao,” alisema Dk. Slaa.
“Wana vitendea kazi vingi na wapo wanazingatia soka la vijana lakini Simba na Yanga ziko pale pale miaka nenda rudi, ni dhahiri kwa mwenendo huu hawatafika.” | 4 |
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ameliagiza Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kushirikiana na Jeshi la Polisi kumkamata na kumweka ndani Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Tumaini Godfrey a.k.a. Dudu Baya kwa kukejeli na kumdhihaki hayati, Ruge Mutahaba.Msanii Dudubaya jana alijirekodi katika clip na kuisambaza mitandaoni akionesha kuulizia wasanii waliokufa siku zilizopita kama Ruge amefika huko, kwani aliwazurumu watu na kawatesa…. Anaelekea kwenye mlango wengi au kapita pembeni aa kumbe wa kushoto…. Akifungua Mkutano wa Kazi wa 11 wa Maofisa Utamaduni nchini uliofanyika jijini hapa, Waziri Mwakyembe alisema, kitendo cha msanii huyo cha kukejeli kifo cha Mutahaba si cha utamaduni wa Watanzania.Dk Mwakyembe alisema huwezi kukejeli kifo cha Ruge, ndio maana hata Rais John Magufuli alikuwa mtu wa kwanza kutwiti akionesha masikitiko makubwa kutokana na kifo cha Mtendaji Mkuu wa Clouds Media, Ruge.“Nimesikitika sana, msanii wa siku nyingi unamkejeli mwenzako, hujui ni Watanzania wangapi wameumia kuhusu kifo hicho... Hujui ukipita barabarani utakuwa salama kiasi gani… Tukakuhifadhi mahali ili akili yako ikae vizuri…ili kumlinda yeye sheria inaturuhusu kabisa. “Mimi naagiza Msaniii huyo achukuliwe hatua kali za kinidhamu … Nami nategemea ndani ya saa mbili awe amechukuliwa hatua.Huu si utanzania tukianza kuruhusu upuuzi huo, haiwezekani… “Nimeumia sana, mwanangu amefanya kazi kubwa ametanguia mbele ya haki, sisi tunakuwa wapuuzi sisi… Hatuwezi kukubali hilo… Hiki ni kipindi cha kuliwazana si kipindi cha kumrushia marehemu vijembe na kuweka madai mbalimbali… Msanii huyo nachokifanya si kizuri.“Kuna watu wameumia sana na mimi mwenyewe nimeumia sana… Huu si utamaduni wa Kitanzania… kufanya hivyo mtu unahatarisha kuondoa amani katika jamii…” Dk Mwakyembe alisema kipindi hiki ambacho watu mbalimbali nchini wanaomboleza kifo cha Ruge kilichotokea Afrika Kusini, msanii huyo amerusha vijembe, kitendo ambacho si kizuri kumrushia vijembe maiti, kitendo hicho kinaweza kuondoa amani kwa jamii.Alisema kutokana na kitendo cha msanii huo ni vema Basata wapeleke malalamiko hayo polisi na ndani ya saa mbili msanii huyo awekwe mahabusu ili kulinda usalama wake. Dk Mwakyembe alisema Ruge ametoa mchango mkubwa katika kuelimisha umma, mchango ambao msanii Dudu Baya anaweza asiutoe hata katika kipindi cha miaka 100 ijayo. Taarifa zingine zilizopatikana baadae jana zinasema kuwa, Dudubaya alijisalimisha mwenyewe katika Kituo cha Polisi Oysterbay, ambako amehifadhiwa. | 4 |
Malkia wa uigizaji katika tasnia la filamu Bongo Move, Irene Uwoya, amewatolea povu wanaohoji mbona hajengi mara kila siku anakula bata amewajibu waendelee kupamba dunia kwa kujenga yeye atapaka rangi kwa bata. Mara nyingi msanii huyo amekuwa akionekana ni mpenda starehe kutokana na maisha yake kuyaweka katika mitandao akionekana anakula bata kila wakati. Msanii huyo ambaye aliwabatiza jina la vichoroko kwa wale wanamfuatilia maisha yake “Vichoroko: Irene mbona haujengi… kila siku bataa haya ni maisha tu kuna kesho,” Uwoya aliandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Instagram akisema kuwa haya ni maisha tu kuna kesho na kama wakijenga wote nani atapanga sio lazima wote wajenge nyunga. “Wengine tutakuwa maua kwa bustani na nyie pambeni tu dunia kwa kujenga sisi tutapaka rangi kwa bata,” aliandika Uwoya. Aliongezea kuwa Vichochoro: “Sio kwamba hatuna pesa ya kwenda hotel au kujionyesha ila tunapenda private life.
Uwoya akijibu”Wenye private life hawaongeagi bali nyie hamna vya kuonyesha,”Uwoya. Vichoroko :Irene mbona hujengi…kila siku bataaa Haya maisha tuuu kuna kesho Me :tukijenga wote nani atapanga?sio lazima wote tujenge …wengine tutakuwa maua kwa bustaniii na nyie pambeni tu dunia kwa kujenga sisi tutapaka rangi kwa bata. Vichoroko :sio kwamba hatuna pesa yakwenda hotel au kujionyesha ila tunapenda private life Me: wenye private life hawaongeagi Bali nyie hamna vya kuonyesha.😷 A post shared by Irene Uwoya (@ireneuwoya8) on Aug 7, 2019 at 2:38am PDT | 1 |
Hadi sasa Tanzania imewekeza katika ukanda huo kwa asilimia 45, huku India ikiwekeza kwa asilimia 21, China asilimia tisa na nchi nyingine mbalimbali kwa asilimia 25. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Uwekezaji, Uhamasishaji na Uwezeshaji wa EPZA, Zawadia Nanyaro jana Dar es Salaam wakati akitoa mafunzo kwa wanahabari kuhusu maeneo ya uwekezaji hapa nchini.Alisema ukanda huo unawatafuta wawekezaji kwa ajili ya kuwekeza katika viwanda ambayo yapo manufaa mbalimbali yanayoweza kupatikana kwa Taifa na hata kwa wananchi. “Lengo kubwa la uwekezaji nchini ni kusaidia katika kukuza ajira mpya, uwekezaji mpya ambao utaongeza fedha za kigeni kwa kuwa bidhaa zitakazozalishwa katika viwanda hivyo zitauzwa nje ya nchi,” alisema Zawadia na kuongeza kuwa uwekezaji huo lazima uwe mpya ndipo atakapopatiwa leseni.Alisema tangu kuanza kwa uwekezaji katika ukanda maalumu hapa nchini yapo maeneo saba ya viwanda, huku mtaji uliowekezwa katika maeneo hayo ni dola za Kimarekani bilioni 1.27 na kampuni ziko 130. Alisema mauzo ya EPZ nje ya nchi yameweza kuingiza fedha za kigeni dola milioni 794 na ajira zilizopatikana ni 31,923.Kuhusu maeneo alisema katika eneo la viwanda lilipo jijini Dar es Salaam, lina ukubwa wa ekari 65 likiwa na viwanja takriban 20 likiwa na miundombinu yote inayohitajika. Kuhusu ujenzi wa miundombinu katika maeneo hayo alisema nchi nyingine serikali zao ndio huhusika na kujenga hivyo ili kuwavutia zaidi wawekezaji. | 5 |
WABUNGE wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (AEAC) kutoka Tanzania, wameeleza njia muafaka ya kuondoa vikwazo visivyo vya ushuru katika jumuiya hiyo ni uanzishwaji wa kamati ya kusimamia biashara.Aidha, wabunge wamepongeza jitihada za serikali katika kuharakisha kupitisha makubaliano, yanayofanywa kwenye jumuiya hiyo, huku ikiwa makini katika kulinda maslahi ya nchi. Pia, wabunge hao wametaka Watanzania kujivunia nchi yao, kwa kuwa na amani, huku Rais John Magufuli akisifika kwa kuhakikisha rushwa inaondoka nchini. Wabunge hao wameitaka Tanzania kuenzi Kiswahili katika EAC na kuhakikisha wimbo wa jumuiya hiyo, unaimbwa katika shule za msingi.Walisema hayo walipozungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kabla ya kuanza ziara ya siku tano nchini Tanzania. Katika ziara hiyo, watakutana na wadau mbalimbali nchini ili kujua vikwazo, mafanikio na nini cha kufanya kwa watanzania katika kukamata fursa za kibiashara zilizopo katika mtangamano wa jumuiya hiyo.Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa waandishi wa habari, kabla ya kuanza ziara hiyo, walieleza bayana kuwa bado kuna changamoto kwa Watanzania kutambua na kukamata fursa zilizopo katika jumuiya hiyo. Mwenyekiti wa wabunge hao, Dk Abdullah Makame (pichani) alisema moja ya changamoto kubwa kwa watanzania na wananchi wengine ndani ya jumuiya hiyo ni kushindwa kuundwa kwa kamati ya kusimamia biashara EAC, ambayo ni utekelezaji wa Ibara ya 24 katika makubaliano ya Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja.“Kuundwa kwa kamati hii kutakuwa mwarobaini wa matatizo, kwani kutapunguza vikwazo visivyo vya kibiashara, kwani itifaki inazungumzia kuwa kila nchi inatakiwa kuwa na wajumbe watatu wenye utaalamu wa sheria na forodha, kwani kazi ya kamati hii kwa sasa inafanywa na mawaziri,“alisema. Alipongeza kazi za kukabili vikwazo zinavyofanywa na mawaziri, lakini kwamba ni vema kuwa na wataalamu.Alisema vikwazo hivyo siyo suala la kuvusha bidhaa pekee, bali pia binadamu kwenda katika nchi nyingine kupata ajira na kupata fursa mbalimbali. Makame alisema katika ziara yao iliyoanza jana, watakutana na wataalamu katika sekta binafsi na ile ya umma, kuona jinsi Tanzania inavyotekeleza makubaliano ya Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja pamoja na changamoto zake.Pia, watakutana na wanafunzi wa vyuo vikuu katika ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Aidha, watapata nafasi ya kukutana na asasi za kiraia, wananchi na wafanyabiashara katika Kituo Kikuu cha Mabasi ya kwenda mikoani na nchi jirani cha Ubungo, Dar es Salaam, ambapo watapata nafasi ya kutoa elimu kwa watanzania kuhusu mtangamano wa EAC.Wakizungumzia tuhuma zinazotolewa mara kwa mara na baadhi ya vyombo vya habari ndani ya EAC, kuwa Tanzania inakwamisha utekelezaji wa makubaliano kadhaa, Mbunge wa jumuiya hiyo, Adam Kimbisa alibainisha kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza, kwa kupitisha na kutekeleza mikataba mingi ya jumuiya hiyo. “Ni vema kueleza kuwa Tanzania ndiyo nchi kubwa katika EAC huku ikiwa ni mmoja wa waanzilishi, kuna baadhi ya maamuzi ni lazima kufanywa kwa umakini sana,” alibainisha Kimbisa.Mbunge mwingine wa jumuiya hiyo, Fancy Nkuhi alisema kuna baadhi ya masuala ya utekelezaji wa makubaliano, yanakuwa shida kutekelezwa kutokana na sheria kuwa tatizo, hivyo ni vema kufanyia kazi ili kurahisisha utekelezaji wake, kwani watendaji wanabanwa na sheria. Alitaka vijana kujitokeza katika mkutano, watakaofanya Jumatano jioni UDSM ili kufahamu namna ya kujiandaa kiutendaji na kutumia fursa zilizopo katika jumuiya.Mbunge Habib Mnyaa alisema Tanzania imejiweka mbali katika kuhakikisha umoja wa EAC unaimarika, kwa wimbo wake kuimbwa kwa ufasaha na watu wake, hivyo kutaka kuanza utaratibu wa kutumika katika shule za msingi. Alisema kwa sasa wimbo huo unaotumia lugha ya Kiswahili, hutumika katika nchi za Rwanda, Burundi na nyingine. Alisema pia bendera ya EAC ni vema ianze kupeperushwa katika wizara zote ili kujifahamisha na siyo kuwapa nguvu wengine.Alisema Tanzania ni mmoja wa waanzilishi wa EAC lakini nadra kuona bendera hiyo. Mbunge Ngwaru Maghembe alitaka watanzania kujivunia kuwa na amani katika ukanda huo. Alisema hivi karibuni walifanya ziara katika kambi za wakimbizi kwenye Jumuiya hiyo na ni Tanzania pekee ambayo haina wakimbizi kwenye makambi.Pia alieleza kuwa Tanzania inajivunia Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli ambaye anasifika katika ukanda huu katika kupambana na rushwa na amedhamiria kuiondoa nchini. Mbunge Pamela Maasay alitaka watendaji kuhakikisha kunakuwa na viwango sawa vya bidhaa katika EAC, ili kuwezesha wananchi kutoka pande zote kuvifuata na kunufaika. Kuhusu uanzishwaji wa Baraza la Vijana EAC, alisema muswada umepitishwa tayari na lengo ni kuwezesha vijana kukamata fursa mbalimbali. | 3 |
Baada ya kuchapisha na kutangaza habari za fursa za kibiashara na uwekezaji zilizopo mkoani Lindi kwa wiki tatu mfululizo, mkoa huo uliopo kusini-mashariki mwa Tanzania umefahamika kidunia, Kaimu Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Tuma Abdallah ameeleza.Akizungumza katika Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji lililoandaliwa na TSN kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa w Lindi, Tuma ameeleza kuwa timu ya wanahabari imezunguka katika wilaya tano za Lindi na kuibua fursa mbalimbali zilizopo.Katika Jukwaa hilo linaloendelea mjini Lindi ambalo limewaleta pamoja wajasiriamali, wafanyabiashara wakubwa na taasisi za kifedha na utendaji wa serikali, Kaimu Mhariri wa TSN amewaeleza washiriki kuwa kampuni hiyo ya Magazeti inarusha taarifa zake kwenye mitandao ya kijamii na Kituo chake cha luninga mtandaoni kupitia mtandao wa YouTube kinachoitwa ‘Daily News Digital’ kinachoonekana duniani kote.Amesema kuwa taarifa zote za fursa katika halmashauri hizo tano na manispaa moja zimechapishwa kwenye magazeti yake ya Daily News na HabariLeo ambayo kwa siku ya leo, Jumanne, husambazwa Afrika Mashariki, hivyo taarifa za fursa za Lindi zimewafikia wawekezaji wa ndani na nje ya Tanzania.Hili ni jukwaa la tisa kufanyika tangu TSN kuanzisha majukwaa mikoani kwa lengo la kuibua fursa za biashara na uwekezaji. Mbali na Lindi, mikoa mingine ambayo imekwishaandaa Jukwaa la Fursa za Biashara ni Tanga, Arusha, Mwanza, Simiyu, Geita, Shinyanga, Tabora pamoja na Zanzibar. | 3 |
VILIO vimetanda katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kuwahukumu kifungo cha maisha jela washitakiwa nane, akiwemo Mwenyekiti wa kitongoji cha Bunju A, Yusuph Sungu (40), baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kuchoma Kituo cha Polisi Bunju A.Washitakiwa wengine waliohukumiwa jana ni Juma Kozo(32), Rashid Liwima(29), Baraka Nkoko(23), Abuu Issa(36), Abraham Mninga(23), Veronica Ephraem(32) na Ramadhani Said(22). Aidha, mahakama hiyo imewaachia huru Mrisho Majaliwa (30), Hamis Ndege (37), Seleman Gwae (33), Menge’nya Anthony (28), Rehema Hussein (32) Rajabu Ally (25), Ally Athuman (24), Amina Matipwili (33), Gubila Temba (51) na Mariam Honza (44).Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alisema upande wa mashitaka ulileta mashahidi 17 kuthibitisha mashitaka hayo. Alisema Kifungu cha 319 A cha Kanuni ya Adhabu, kinaeleza kwamba washitakiwa wanaotiwa hatiani kwa makosa hayo, adhabu ni mpaka kifungo cha maisha na kwamba mahakama yenyewe itaamua ni aina gani ya adhabu ya kuwapa washitakiwa.Hakimu Simba alisema mahakama hiyo ilienda eneo la tukio na kwamba waliona kilivyoteketea kwa moto, ikiwa ni pamoja na bunduki na vifaa vyote vya kituoni hapo na kwamba waliona damu, hivyo inawezekana kulikuwa na mahabusu. “Kitendo hiki ni cha kinyama na sio tu hujuma, hivyo mahakama inawahukumu kifungo cha maisha hela,” alisema Hakimu Simba.Alisema kwa mara ya kwanza washitakiwa hao walikuwa 35, lakini waliachiwa 17 na 17 walikutwa na kesi ya kujibu. Hakimu Simba alisema ni ukweli usiopingika kuwa kituo hicho, kilichomwa na kwamba hakukuwa na tatizo la umeme na kwamba sababu ni watu kukusanyika kutokana na kifo cha mtoto aliyegongwa na gari. Alisema pia ni ukweli kwamba kila kitu kilichokuwepo kwenye kituo hicho, kiliteketea kwa moto na magari yalipigwa mawe.“Mwenyekiti alichochea wananchi waliozingira kuchoma moto kwa kituo hicho kwa kutumia mafuta ya petroli,” alisisitiza. Kabla ya kutolewa adhabu, Wakili wa Serikali, Ester Martin alidai kosa walilolifanya washitakiwa hao ni kubwa na ambalo linahatarisha usalama, hivyo linastahili kulaaniwa na yoyote.Alidai tukio hilo linahatarisha amani na kuleta taharuki kwa raia wasio na makosa, hivyo mahakama itoe adhabu kali kwa watuhumiwa hao kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwa wenye tabia hiyo.Hata hivyo, washitakiwa hao waliomba mahakama iwapatie kifungo cha nje au kulipa faini kwa sababu wanategemewa. Baada ya hukumu hiyo, vilio vilitanda mahakamani hapo kwa mshitakiwa Veronica akiwalilia watoto wake, huku ndugu wa washitakiwa hao kutoamini kilichotokea, kwa kuwa walikuwa nje kwa dhamana.Washitakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na mashitaka sita, ambayo waliyatenda Julai 10,2015 maeneo ya Bunju A wilayani Kinondoni. Washitakiwa hao wanadaiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kuharibu mali ikiwemo magari manne, ambayo walipasua vioo na kuchoma moto kituo hicho, mali ya Jeshi la Polisi na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. | 3 |
Na Joyce Kasiki, Dodoma Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili na Utalii, Nape Nnauye amesema anatamani bunge lisiwe la kutunga sheria tu bali pia lifute sheria za hovyo au kuzirekebisha. Pia Nape ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kufanya uchambuzi wa sheria zake na kuangalia namna ya kuondoa sheria kandamizi katika sekta ya utalii ili taifa linufaike na rasilimali zilizopo katika sekta hiyo. Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo Mjini Dodoma leo Jumatano Machi 28, Nape amesema zipo sheria ambazo ni kandamizi hivyo wizara inapaswa kuzichambua na kupeleka bungeni ili ziondolewe au zifanyiwe marekebisho. “Fanyeni uchambuzi wa sheria kandamizi, mi natamani bunge lisiwe la kutunga Sheria tu ,bali pia lifute Sheria za hovyo au kuzirekebisha,” amesema Nape. Aidha, ameitaka wizara hiyo kuongeza vigezo vya kupima madhara ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika sekta ya utalii lakini pia kutoa taarifa ya uchambuzi wa kodi mbali mbali katika wizara hiyo. “Naomba tusijpe muda mrefu wa kupima madhara ya VAT, wenzetu Kenya wameshafuta hiyo, sasa hadi wamefuta wao si wajinga,” ameeleza. | 3 |
LEONARD
MANG’OHA-DAR ES
SALAAM MKUU wa
Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro, ameagiza kukamatwa kwa mtu anayedaiwa kuwa
ni mume wa mtangazaji maarufu nchini, Zamaradi Mketema, ambaye ametajwa kwa
jina la Shaban kwa tuhuma za kumtishia
dereva mwenzake silaha aina ya bastola. Akizungumza
Dar es Salaam jana, Sirro alisema kuwa watu hupewa silaha kwa masharti maalumu
na kwamba hawakuwapa ili wawatishie Watanzania. IGP Sirro
alisema tayari Jeshi la Polisi linamsaka kijana huyo licha ya kwamba amekuwa
akiwakwepa kwepa. Kauli ya IGP
Sirro imekuja siku moja baada ya juzi jioni kusambaa video inayomwonesha Shaban
aliyekuwa na gari dogo lenye rangi ya bluu akitishia kumpiga risasi dereva
mwenzake aliyekuwa akiendesha gari kubwa. IGP Sirro
alisema kuwa licha ya kutofahamu sababu ya ugomvi uliosababisha kijana huyo
kutoa silaha lakini suala la kujiuliza ni kama kulikuwa na ulazima kumtishia
silaha. “Tukibaini
umetishia Watanzania kama alivyofanya yule kijana, hatujui ugomvi ulikuwa ni
nini lakini je, kama ni kweli yale yaliyokuwa yanaelezwa kulikuwa na ulazima wa
kutoa silaha kumtishia mwenzake?” Alihoji IGP Sirro . “Kimsingi
mtu ukipewa silaha hakikisha unafuata yale masharti, usipofuata masharti la
kwanza tutakunyang’anya silaha, lakini la pili tutakupeleka mahakamani na la
tatu tutamwomba Mungu tukufunge ili ukirudi nyumbani kwa mke wako au kwa mume
wako uwe na adabu ya kutunza vitu vyako,” alisema IGP Sirro. Katika video
hiyo dereva wa gari kubwa alianza kusikika akimwambia dereva wa gari dogo (Shaban)
kuwa; “umesema unatoa bunduki itoe hiyo
bunduki,”. Wakati mzozo
huo ukiendelea dereva wa gari dogo (Shaban) aliyekuwa amevaa shati jeupe
alielekea kwenye gari lake na kutoka na bastola. Licha ya
dereva huyo kutoka na bastola yule wa gari kubwa ambaye alisikika akiongea kwa
jazba hakuonesha kutishika na kitendo cha mwenzake kutoka na bastola na
kumwambia kuwa kama anataka kumshambulia kwa bastola haogopi kwa sababu
alizaliwa ni lazima atakufa. “Mimi kufa
nitakufa na wewe utakufa, huna lolote nakwambia kweli huna lolote, toa hiyo
bunduki, mwache aniue,” alisikika akisema dereva wa gari kubwa. Licha ya
dereva wa gari dogo kumwamuru mwenzake akae chini huku akitukana matusi bado
dereva huyo alikataa huku akisisitia kuwa kama anataka amuue. Pia dereva
huyo alionekana akimpiga mwenzake na bastola hiyo kichwani na kumweleza kuwa
atampasua kwa kutumia silaha hiyo aliyokuwa ameishika. Juhudi za
gazeti hili kumtafuta Shaban ziligonga mwamba. Zamaradi
alipotafutwa kwa simu kuzungumzia kuhusu video hiyo na kama mtu anayeonekana
humo ni mume wake, simu yake iliita bila kupokewa na hata alipotumiwa ujumbe
mfupi wa maandishi kwa njia ya mtandao wa Whatsapp licha ya ujumbe huo kusomwa
haukujibiwa. Mmoja wa
watu wa karibu na mtu huyo aliyetajwa kwa jina la Shaban ambaye hakutana jina
lake liandikwe gazetini alithibitisha kuwa ni kweli kijana huyo ni mume wa
Zamaradi. | 3 |
WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema Sheria ya Huduma za Habari inayoanza utekelezaji mwaka huu itawabana wamiliki wa vyombo vya habari wanaowatumia waandishi bila kuwa na mkataba wa ajira.Alisema ni jambo la kushangaza kuona waandishi wa habari wanafanya kazi kwa miaka mingi bila kuajiriwa akichukulia mfano wa manamba.Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam katika semina ya haki za binadamu, maadili na utayarishaji wa vipindi iliyoandaliwa na Kampuni ya Mac D Promotion, Dk Mwakyembe alisema wanapoanza utekelezaji wa sheria hiyo namba 12/2016 vyombo vingi vya habari vitatikisika.“Ni heri kuwa na waandishi watatu kwenye chombo kimoja cha habari kuliko kuwa na waandishi 50 ambao wanafanya kazi kama manamba. Waandishi wengi wakiacha kazi wanarudi majumbani kama walivyo, hilo hatutakubali ni lazima haki za wafanyakazi zifuatwe,” alisema. Alisisitiza utekelezaji huo utasaidia kuwepo kwa baraza huru la habari, kuunda chombo cha malalamiko ambacho kitakuwa mfano wa mahakama na wataunda mfuko wa waandishi wa habari kwa ajili ya kuwasomesha nje ya nchi. Pia alivitaka vyombo vya habari nchini kujenga madaraja ya mawasiliano na serikali na si taasisi za nje. Alieleza serikali ndio yenye uwezo wa kusaidia vyombo vya habari vya ndani kupata habari sahihi na si taasisi au wafadhili kutoka nje ya nchi.Dk Mwakyembe alisema serikali ipo bega kwa bega na vyombo vya habari ili wananchi waweze kupata habari zilizo makini. Mkurugenzi wa Kampuni ya Mac D Promotion, Deogratius Rweyunga alisema kampuni hiyo imekuwa mstari wa mbele kutoa mafunzo kwa wanahabari nchini ili waweze kupata uzoefu katika kazi zao. Alisema mambo ya kuzingatia ambayo waandishi wa habari wanatakiwa kuyafanya ni kufuata maadili na kutumia kalamu zao vizuri kuleta maendeleo na si kubomoa. Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga aliwataka waandishi wa habari kuandika habari zinazomlenga mwananchi moja kwa moja kwa kuzingatia maadili. Alisema ni lazima kuwe na muendelezo wa habari na kufanya habari za uchunguzi ili kuibua matatizo na kuyatafutia ufumbuzi.Henga alisema Katiba ya Tanzania ibara ya 18 inaeleza kuhusu haki za uhuru, kutoa na kupata habari ambayo ni ibara nzuri kuliko zote zilizopo Afrika Mashariki. Mwezeshaji wa semina hiyo Allan Lawa ambaye pia ni mjumbe wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), alisema ni lazima kuachana na uandishi wa habari wa mazoea, badala yake kuandika habari zitakazosaidia kuondoa matatizo katika jamii. | 3 |
Okwi anayechezea Simba, anatarajiwa kwenda nchini Denmark kufanya majaribio katika Klabu ya Sonderjyske inayoshiriki Ligi Kuu ya huko kuanzia kesho.Kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya Klabu ya Simba jana, majaribio hayo yatakuwa ya siku 14 kuanzia kesho na baada ya hapo klabu hiyo ya Sonderjyske itatuma ripoti kamili ya majaribio hayo.Rais wa Simba, Evans Aveva alisema: “Simba inafurahi sana kuona wachezaji wake wanapata nafasi hizi za kuonesha vipaji vyao tena kwenye viwango vya kimataifa zaidi, hivyo Simba inamtakia kila la kheri Okwi kwenye majaribio yake ya siku 14 kwenye Klabu ya Sonderjyske iliyopo kwenye ligi ya Denmark.”Okwi aliyezaliwa miaka 23 iliyopita nchini Uganda, aliwahi pia kucheza kwa muda mfupi katika Klabu ya Etoile Sportive du Sahel ya Tunisia na baadaye kuichezea Yanga kabla ya msimu uliopita kurudi klabu yake ya Simba.Katika hatua nyingine, mshambuliaji na nahodha wa Azam FC, John Bocco mambo yake yamemnyookea baada ya Klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini kukubali kumsajili.Taarifa zilizopatikana kutoka vyanzo mbalimbali vya habari, Azam FC imekubali kumuuza mchezaji huyo na kinachosubiriwa ni timu hiyo kumalizana juu ya maslahi binafsi ili kuhamia katika timu hiyo.Kwa mujibu wa mtandao wa bongostaz, Azam FC imekubali kumuuza mshambuliaji huyo kwa kitita cha Dola za Marekani 80,000 ikiwa ni sawa na zaidi ya Sh milioni 160,000 kwa klabu hiyo.Na sasa kinachosubiriwa na Free State kumalizana na mchezaji juu ya maslahi binafsi ili mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tanzania, ahamie Ligi Kuu ya ABSA Afrika Kusini.Mshambuliaji mahiri, Mrisho Ngassa aliyesajiliwa na Free State miezi miwili iliyopita baada ya kumaliza mkataba Yanga, anaeleza kuwa ndiye aliyempa ulaji huo Bocco kwa kuwapa viongozi wa timu hiyo mawasiliano ya Bocco.Hata hivyo, gazeti hili lilipomtafuta Msemaji wa Azam FC, Jaffari Idd kuzungumzia taarifa hizo, alisema hazina ukweli na kama zitakuwa na ukweli zitawekwa mara moja katika tovuti ya klabu hiyo.Bocco aliwahi kufanya majaribio Afrika Kusini katika Klabu ya Supersport na Algeria na kufuzu ila hakuuzwa kutokana na dau dogo | 4 |
KINSHASA, DRC SERIKALI ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imewafukuza kazi zaidi ya mahakimu 250 waliokuwa wameajiriwa kwa kutumia vyeti feki na wengine waliotuhumiwa kupokea hongo. Tume maalumu iliundwa kufuatilia maofisa katika idara mbalimbali, ambao hawana sifa ya kufanya kazi ya uhakimu au nyinginezo za kitaalamu serikalini. Rais Joseph Kabila aliwafukuza kazi mahakimu hao kwa kile alichosema kosa kutumia vyeti bandia na wengine kwa tuhuma za kupokea rushwa wakati wa kesi mbalimbali. Hatua hii inafuata malalamiko mengi ya wananchi pia kutokana na utendaji wao mbovu. Mara kwa mara mashirika ya kiraia yamekuwa yakilalamika utendaji wa mahakama na hatua ya kuwatimua inaonekana kuwa moja ya majibu hayo, anasema Dufina Tabu mratibu wa Shirika la Kutetea Haki za Binaadamu nchini Congo (Savoco). ‘Tulikuwa tukimwandikia Rais barua na inaonekana zimefika. Kwa hivyo inakuwa ni mfano mzuri. ‘Maskini kupata haki yake kisheria ni vigumu. Kila kitu ni fedha. Watu wanateswa kupata haki na tutaendelea kumwunga mkono Rais. Kwa yoyote atakayefanya makosa tutamwandikia, tumtaje na aadhibiwe kabisa ili tuweze kuisaidia nchi yetu ipone’, alisema. Hata hivyo, Waziri wa Sheria Alexi Tambwe Mwamba amesema tume maalum iliyoundwa kuendesha uchunguzi zaidi ya mahakimu ndiyo iliyogundua uwapo wa mahakimu feki. Mara kwa mara rais Kabila ametangaza kuchukua hatua kukabiliana na rushwa nchini hapa, lakini wakosoaji wamekuwa wakiona hakuna ishara wala azma ya kisiasa na uthibitisho wa hatua kupigwa katika kukabiliana na hilo, mbali ya kuundwa sheria kali, ambazo mara nyingi hazifuatwi. Shirika la Kimataifa la Kutetea haki za Binadamu, Transparency International linasema ajenda ya kupambana na rushwa mara nyingi huingiliwa kati kwa maslahi ya kisiasa. Rasilmali ni finyu kwa mahakama za nchi hiyo ambayo imeshuhudia vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda sasa. Na hiyo inamaanisha kuwepo kwa maafisa wasiotosha kukabiliana na mzigo wa mahitaji na pengine ndio kukatoa mwanya wa kuajiriwa majaji hao 250 hewa. | 2 |
KOCHA wa AFC Leopards Casa Mbungo ameondoka klabuni hapo baada ya kusitisha mkataba wake. Kocha huyo mnyarwanda jana alikwenda mazoezini na kuwaaga wachezaji na wafanyakazi wenzake.“Nitawakumbuka, nitaikumbuka Kenya. Tafadhali endeleeni kufanya kazi kwa bidii, hamuwezi kujua kitakachokuja mbele,” Mbungo aliwaambia wachezaji wake.Mbungo ameondoka kwenye klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Kenya kutokana na kukumbwa na ukata. Amelazimika kusitisha mkataba wake baada ya kutolipwa mshahara wake kwa miezi mitano na huku akidaiwa kudai malimbikizo ya mshahara wake zaidi ya sh milioni mbili za Kenya.Ametoa siku 15 kwa klabu hiyo kumlipa fedha zake vinginevyo atawashitaki kwa Shirikisho la soka la kimataifa, Fifa. AFC Leopards kwa siku za karibuni imekumbwa na ukata na haijalipa wafanyakazi wake tangu SportPesa ilipositisha mkataba nao tangu Agosti mwaka huu.“Inasikitisha safari hii kuisha hivi, tumejifunza mengi kutoka kwako, yatabaki kwenye fikra zetu, Mungu akuvariki kocha Andre Casa Mbungo,” alisema nahodha wa timu hiyo Robinson Kamura.Kocha msaidizi Anthony Kimani anatarajiwa kuiongoza Leopards katika mechi ya mwishoni mwa wiki dhidi ya Zoo Kericho mjini Kakamega | 4 |
NAIROBI, KENYA WAZIRI wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Dk. Fred Matiang’i amesema mwanasiasa wa upinzani aliyetimuliwa nchini Kenya, Miguna Miguna atalazimika kuomba tena uraia. Waziri huyo amesema Miguna alipoteza uraia wake alipochukua wa Canada mwaka 1988, hivyo hawezi kuruhusiwa kuingia Kenya kama raia bila kuomba tena uraia. Dk. Matiang’i aliyekuwa akihojiwa na Kamati ya Bunge, amesema mwanasiasa huyo ambaye pia ni wakili alijipatia pasipoti na kitambulisho cha taifa anachokitumia sasa kwa njia ya ulaghai. Waziri huyo amesema hakuna anayepinga Miguna alizaliwa Kenya. “Yeyote aliyechukua uraia wa taifa lingine kabla ya Katiba ya sasa kuidhinishwa mwaka 2010, ambaye anafikiri anaweza kuitumia bila kufuata utaratibu uliowekwa anajidanganya. “Hapana shaka Miguna alizaliwa Kenya. Lakini kwa mujibu wa Katiba ya kabla ya 2010, yeyote aliyechukua uraia wa nchi nyingine alipoteza uraia wa Kenya. Bunge liliidhinisha sheria inayoeleza jinsi mtu wa aina hiyo anavyoweza kupata tena uraia wake.” Alisema. Waziri huyo pia alijitetea dhidi ya shutuma kuwa amekuwa akikaidi maagizo ya mahakama ya kutaka Miguna aachiwe huru na kuruhusiwa kuingia Kenya. Jaji wa Mahakama Kuu, George Odunga alikuwa ameagiza Dk. Matiang’i, pamoja na Mkuu wa Polisi, Joseph Boinnet, Mkuu wa Uhamiaji Gordon Kihalangwa na Katibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Karanja Kibicho wafike mbele yake kueleza ni kwa nini walikaidi amri ya mahakama ya kumruhusu Miguna aingie Kenya. Dk. Matiang’i amesema: “Jaji alipokuwa anatutaka tufike mbele yake tulikuwa tunahudhuria sherehe za kufuzu kwa maafisa wa polisi wa kukabiliana na ghasia (GSU). Tulihukumiwa bila kupewa fursa ya kujieleza, kwa kutumia madai ya uongo,” alisema. Jaji Odunga aliwapiga faini ya shilingi mia mbili kila mmoja na akaagiza pesa hizo zikatwe kutoka kwenye mishahara yao. Dk. Matiang’i pia alipuuza madai kuwa serikali ilimfurusha Miguna kutoka Kenya akisema hatua kama hiyo ingehitaji idhini yake. “Hakufurushwa kutoka Kenya. Nilihitaji kutia saini idhini ya kumfurusha. Hatungemfurusha kwani hakuwa ameingia bado ndani ya eneo la utawala wetu. “Tulimuondoa uwanja wa ndege kama mtu ambaye hakuwa na nyaraka za kumtambua, abiria ambaye hangetambuliwa ambaye kawaida hurejeshwa alikotoka,” alisema Dk. Matiang’i. | 2 |
Waziri Mkuu Majaliwa alisema kwa sasa serikali imejipanga katika msimu huu wa kilimo mazao yote ya biashara kuuzwa kupitia vyama vya ushirika. Kutokana na hilo, amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha vyama hivyo vinakuwa na viongozi waadilifu na waaminifu.“Wakuu wa mikoa hakikisheni vyama vya ushirika vinakuwa na watu makini, simamieni ushirika ili uwanufaishe wananchi," alisema na kuongeza kuwa hatua ya kuuza mazao kupitia vyama vya ushirika itasaidia wakulima kutolaliwa na wafanyabiashara pindi watakapotaka kununua kwa bei ndogo.Aidha, ameitaka jamii kujenga utamaduni wa kuhifadhi chakula katika ngazi ya kaya. Alisema serikali imedhamiria kwa dhati kuongeza uwezo wa uhifadhi wa chakula kuweza kufikia tani laki 700,000 ifikapo mwaka 2025. Pia aliwataka wananchi kutumia fursa ya mvua zinazonyesha kulima mazao mengi.Akizungumza kwa niaba ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mahmoud Mgimwa aliitaka serikali kuiangalia kipekee Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).Mgimwa alisema kama serikali haitaongeza fedha, maghala na vihenge vinavyojengwa havitakuwa na tija. Alisema ujenzi huo utakuwa na tija kama fedha zilizoombwa na NFRA katika bajeti yake zitatolewa.Mwenyekiti huyo alisema katika mwaka wa fedha 2018/19, Wakala huo umeomba kiasi cha Sh bilioni 86 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo kununua mazao ya wakulima.Waziri wa Kilimo, Dk Charles Tizeba alisema changamoto wanazokutana nazo ni pamoja na katika msimu wa mvua waliingia panya na wadudu aina ya viwavijeshi ambao alidai wamekuwa wakila mazao ya wakulima.Alisema wamejipanga kukabiliana nao kwa kuwataka wakurugenzi kutoa taarifa pindi wanapoona panya hao kwa wizara yake ili dawa ya kuwazuia itumwe.Kaimu Mtendaji wa NFRA, Vumilia Zikankuba alisema mradi huo utatekelezwa katika maeneo nane ya wakala ambayo ni Songea, Makambako, Mbozi, Sumbawanga, Mpanda, Shinyanga, Dodoma na Babati. Zikankuba alisema NFRA inamiliki maghala ya kuhifadhi nafaka 34 yenye uwezo wa kuhifadhi tani 251,000.Alisema uwezo huo wa sasa hautoshelezi mahitaji ya dharura ya chakula kwa mfululizo wa miezi mitatu kwa akiba isiyopungua tani 700,000, hivyo kuwapo uhitaji wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi. | 5 |
BAADA ya Serikali kununua korosho zote kwa wakulima mikoa ya Kusini, Lindi, Mtwara na Ruvuma, imeanza kushughulikia zao la mahindi katika mikoa ya Ruvuma, Njombe, Iringa, Songwe na Mbeya.Tanzania ni mzalishaji mkubwa wa mahindi Afrika Mashariki katika mikoa tajwa, lakini imeelezwa mahindi hayo kwa kiasi kikubwa yamekosa soko baada ya lile la ndani kujitosheleza kwa chakula.Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, alilieleza gazeti hili jana serikali imeshatuma timu ya wataalamu wake mikoa hiyo ili kutathmini kiasi cha mahindi kilichopo na wakati huo huo kuna timu ya wataalamu inayoendelea kufanya tathmini ya masoko ya zao hilo kwa nchi jirani ili kusaidia upatikanaji wa masoko.Alisema nchi zilizoonesha nia ya kutaka kununua mahindi kutoka Tanzania ni pamoja na Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), lakini pia serikali inawatumia mabalozi wake walioko nchi jirani kama vile Kenya na Sudan Kusini kufuatilia kama nako wanaweza kupata soko la mahindi hayo.“Timu tuliyounda inajumuisha wataalamu kutoka taasisi za Serikali, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade) na Bodi ya Mazao Mchanganyiko; tumewapa wiki moja na nusu watueleze tuna tani ngapi za mahindi nchini,”alieleza Waziri Hasunga.Alisema hivi sasa kuna ziada ya mazao ya chakula ya asilimia 123 na lengo la serikali ni kuliongezea thamani zao la mahindi kabla ya kuyauza nje kupata pato zuri zaidi lakini kutokana na uhaba wa viwanda au mashine ya kuliongezea thamani, kuna baadhi ya nchi yatauzwa mahindi na nyingine utauzwa unga.Mbunge wa Tunduru Kusini mkoani Ruvuma, Daimu Mpakate, alilieleza HabariLeo kuwa ni vyema serikali ikalitumia vyema soko la mahindi Malawi kwa kuitumia Bodi ya Mazao Mchanganyiko.Alisema Ruvuma ina zaidi ya tani milioni 1.5 za mahindi, lakini Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), uwezo wao wa kununua mahindi hayo siyo zaidi ya tani 30,000 hivyo kuhitaji kusaidiwa.Alisema kwa kuwa NFRA wananunua mahindi kwa hifadhi ya taifa na siyo kwa ajili ya biashara kama bodi nyingine, ni vyema serikali ikaiongezea uwezo Bodi ya Mazao Mchanganyiko kununua mahindi ya wakulima na ikiwezekana wayaongezee thamani kwa kutengeneza unga na kisha kuuza nchini Malawi.Alisema ingawa NFRA wananunua mahindi kwa Sh 500 kwa kilo, kutokana na uwezo mdogo wa kifedha , wakulima wanalazimika kuuza kwa wanunuzi binafsi kwa wastani wa Sh 200-270 kwa kilo. | 3 |
Kampuni inayotoa huduma ya usafiri wa Taxi jijini Dar es Salaam, Uber Tanzania iko kwenye mchakato wa kufungua vituo kwa ajili ya kuhudumia wateja wasiokuwa na ‘smartphone’. Mkurugenzi wa Uber Tanzania, Alfred Msemo amesema vituo hivyo ni maalumu kwa wateja ambao hawana smartphone au ambao simu zao zimeisha chaji na kuzimika au ambao hawajui namna ya kutumia huduma hiyo kwenye simu ambapo watasaidiwa na wahudumu watakaokuwapo eneo hilo kuomba huduma ya usafiri bila malipo. “Uber ni huduma ya usafiri wa kuaminika, bei nafuu na salama na katika kuwajali wateja wetu ambao wakati mwingine wanakuwa wameishiwa chaji kwenye simu au hawana smartphone na wanahitaji huduma lakini wanashindwa kutokana na sababu hizo au nyingine,” amesema Msemo. Pamoja na mambo mengine, Msemo amesema kupitia huduma ya Uber wamefanikiwa kutengeneza ajira zaidi ya 1,000 kupitia madereva waliojisajili na Uber tangu kuanzishwa kwake nchini Juni, mwaka jana. “Pamoja na mafanikio hayo ziko changamoto zinazotukabili ikiwamo zikiwamo kuhitajika zaidi mikoani ambako tunatarajia kuanza kusambaza huduma hiyo ili kuwaridhisha wateja wetu,” amesema. Kwa upande wake Ofisa Uhusiano wa Uber, Janeth Kimboi amesema kampuni hiyo inatoa huduma katika nchi 80 duniani ambapo kwa Afrika nchi inayoongoza ni Afrika Kusini ambapo Uber ilianzishwa mwaka 2013, Nairobi mwaka juzi na Dar es Salaam, mwaka jana. Uber ni huduma ya usafiri inayotolewa kupitia programu iliyounganishwa kwenye simu ili kumuwezesha mteja kufanya mawasiliano na dereva aliye karibu na eneo alilopo mteja kupitia ramani maalumu ya google baada ya kuomba huduma hiyo. | 3 |
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM KWA mara ya kwanza Hospitali ya Aga Khan imeanza kufanya upasuaji wa kupandikiza matiti kwa wanawake wasiokuwa nayo baada ya kukatwa ili kutibiwa saratani ya matiti. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Bingwa wa Upasuaji wa Hospitali ya Aga Khan, Dk. Aidan Njau. Alisema madaktari wa Aga Khan watafanya upasuaji huo kwa kushirikiana na madaktari wenzao kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na Shirika la Kimataifa lisilo la Serikali la Women for Women la nchini Marekani. Pia alisema tayari wanawake wawili wameandaliwa kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji huo wa aina yake. “Ni awamu ya tatu sasa tunafanya upasuaji kwa akina mama, watoto na mabinti waliopata madhara katika miili yao kutokana na ajali mbalimbali, lakini kwa upande wa upandikizaji matiti huu ni upasuaji wa kwanza tunaanza kufanya hapa nchini,” alisema na kuongeza: “Tunachofanya ni kutengeneza viungo vyao ili virudi katika hali ya kawaida ili na wao waweze kuendelea na maisha yao kama watu wengine. “Mara nyingi mtu anapoelezwa kuwa ana tatizo la saratani wengi huathirika kisaikolojia na mama anapofanyiwa upasuaji wa kuondoa titi kama sehemu ya matibabu dhidi ya saratani huzidi kuathirika kisaikolojia. “Maumivu huongezeka pale anapoelezwa kuwa matibabu ni kuondolewa ziwa lake kama sehemu ya matibabu, hivyo tunaona upasuaji huu utawafaa na utawasaidia wengi ambao walipoteza kiungo hicho. “Tunachofanya, tunachukua sehemu katika mwili wake na kutengeneza titi ambalo tutakuja kulipandikiza tena kwenye mwili wake, ingawa haitakuwa kama ziwa ambalo Mungu alimpatia, lakini litamwezesha kuwa kama wanawake wenzake”. Naye Mkurugenzi wa Kitengo cha Ajali za Moto na Viungo vilivyokakamaa wa MNH, Dk. Edwin Mrema, alisema pamoja na upasuaji huo, wameandaliwa takribani wagonjwa 33 watakaofanyiwa upasuaji wa kurekebisha viungo. “Baada ya upasuaji tunaendelea kuwafanyia mazoezi, kuna wagonjwa wapo nyumbani wanaishi kwa woga wakiogopa macho ya watu, tunatoa wito watu wajitokeze tuwatibu, ni huduma endelevu,” alisema. Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka Shirika la Women for Women, Andrew Pusic, alisema: “Nafurahi kuwapo Tanzania, tunachofanya ni ushirikiano wa pamoja ili kuweza kuwasaidia wanawake wenye shida mbalimbali na kutoa mafunzo kwa njia ya upasuaji.” | 3 |
RAIS John Magufuli atakuwa na ziara ya kikazi mkoani Mtwara wiki ijayo, ambayo itahusisha uzinduzi pamoja na uwekaji na mawe ya msingi katika miradi mbali mbali ya maendeleo mkoani hapa.Hayo yalielezwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa wakati alipowasilisha taarifa hiyo kwa waandishi wa habari mkoani hapa kuhusu ujio huo wa Rais Magufuli, Aprili 2 hadi Aprili 4, mwaka huu. Kwa mujibu wa Byakanwa, miradi hiyo ni mikubwa ambayo itaenda kuchochea uchumi mkubwa kwa mkoa huu kupitia miradi hiyo na kisha kuleta tija kwa maendeleo ya mkoa huo na Taifa kwa ujumla.Byakanwa alisema kwamba Aprili 2, mwaka huu, Rais Magufuli anatarajia kufungua na kuweka mawe ya msingi ikiwemo kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara, ujenzi wa barabara ya Mtwara hadi Mnivata na kiwanda cha kubangua korosho cha Yalin mkoani hapa. Aidha, alisema Aprili 3, mwaka huu, kiongozi huyo wa nchi ataweka jiwe la msingi kwenye uboreshaji wa miundombinu ya Chuo cha Ualimu Kitangali wilayani Newala.Pia ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mbonde wilayani Masasi pamoja na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wilayani humo. Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Aprili 4, mwaka huu, atafanya uzinduzi wa mradi wa barabara ya Mangaka hadi Nakapanya kuelekea Tunduru na Mangaka hadi Mtambaswala.Mkuu huyo wa mkoa amewaomba wananchi mkoani hapa kujitokeza kwa wingi kwenye mapokezi kwani ujio huo wa Rais Magufuli ni moja ya upendeleo kwa wana-Mtwara. “Ujio huu wa Mheshimiwa Rais Magufuli ni fursa na upendeleo mkubwa kwa mkoa wetu na wana-Mtwara kwa jumla kwani hii ni mara ya pili Mheshimiwa Rais kutembelea mkoa wetu wa Mtwara,” alisema Byakanwa. | 3 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.