text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
Juhudi za karibuni kuimarisha uhusiano huo, zimeshuhudiwa wiki hii ambapo wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka nchi hiyo kubwa kiuchumi Afrika walitembelea nchini kwa mazungumzo zaidi.Ujumbe huo ulihudhuria semina kuhusu biashara kati ya nchi hizo iliyofanyika juzi jijini Dar es Salaam, ambayo ilitayarishwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini.Akizungumza na waandishi wa habari baada ya semina hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Juliet Kairuki, alisema mazungumzo yao yalilenga kuangalia namna nchi hizo zitakavyofaidika kwa kuboresha ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji.Wawekezaji hao kutoka Afrika Kusini, wameonesha nia ya kuwekeza kwenye sekta ya kilimo na kuchagua mikoa ya Mwanza na Morogoro kama maeneo ambayo wangependa kuwekeza.Semina ya biashara ya wiki hii ni matunda ya Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa lililofanyika mkoani Mwanza Februari mwaka huu.Baada ya kongamano hilo, Balozi wa Afrika Kusini hapa nchini, Thanduyise Chilliza ambaye alichukua hatua na kuwa mjumbe wa kutangaza fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania kwa wawekezaji katika nchi yake.Kairuki alisema kwa kushirikiana na Afrika Kusini, Tanzania itafaidika na teknolojia mpya, masoko, uongozi na usimamizi wa miradi mikubwa ya kilimo miongoni mwa faida nyingine.Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera alisema amejifunza mengi katika semina hiyo.“Tumejifunza mengi kutoka kwa hawa wenzetu wa Afrika Kusini hasa katika masuala ya kilimo cha mboga na viungo,” alisema Mkuu wa Mkoa.Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Radhia Msuya, alisifu semina hiyo na kusema TIC imefanya kazi nzuri. “Semina hii imetufungua macho katika mambo mbalimbali,” alisema.Meneja Mtendaji, Export Development and Promotion, Trade and Investment KwaZulu Natal, Lester Bouah alisema ni kwa kushirikiana pamoja ndipo fursa zitapatikana na maendeleo ya kweli kufikiwa. | 5 |
JUMLA ya mabalozi 50 wanaoziwakilisha nchi zao nchini pamoja na viongozi wa mashirika ya kimataifa na taasisi za fedha wanatarajiwa kuhudhuria katika sherehe za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar zitakazofanyika Pemba, kesho kutwa.Akizungumza na baadhi ya mabalozi wadogo waliopo Zanzibar, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika Ofisi ya Zanzibar, Mohamed Haji Hamza ameisema maandalizi ya ujio wa mabalozi hao kwa ajili ya safari ya Pemba yamekamilika.Amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imejipanga kuona kwamba sherehe hizo zinafanikiwa na kuhudhuriwa na viongozi wenye hadhi ya kibalozi.Hamza alisema usafiri wa mabalozi na wakuu wa mashirika ya kimataifa umeandaliwa kuanzia Tanzania Bara hadi watakapofika Zanzibar na tayari kwa safari ya Pemba.Aidha alisema wapo mabalozi watakaofunga safari moja kwa moja kutoka Dar es Salaam hadi Pemba na kurudi ambapo usafiri umetayarishwa.“Maandalizi ya safari ya sherehe za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar yamekamilika ambapo tunatarajia jumla ya mabalozi 50 pamoja na wakuu wa mashirika ya kimataifa na taasisi za fedha watafunga safari kwenda Pemba,” alisema.Alisema hiyo ni moja ya fursa kubwa ya mabalozi kuona mandhari ya kisiwa cha Pemba ambao wapo watakaopata nafasi ya kutembelea baadhi ya vivuto vya utalii.Mapema Naibu Katibu mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Abdallah Hassan Mitawi aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuhudhuria sherehe hizo ambazo ni matokeo ya wananchi wa Zanzibar kufanya Mapinduzi yaliyoung'oa utawala wa Kisultani na wazalendo walio wengi kushika hatamu ya madaraka.Amesema ni miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo mafanikio makubwa yamefikiwa ikiwemo ya kiuchumi, sekta ya elimu na afya pamoja na mawasiliano ya miundo mbinu.“Wananchi wa Zanzibar wanayo kila sababu ya kusherehekea miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo ndiyo yaliyowaweka madarakani wananchi.”amesema. | 3 |
Alitoa ombi hilo jana mjini Songea kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipofanya ziara katika Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) Kituo cha Songea kukagua kazi ya ununuzi wa mahindi akiwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Ruvuma.Alisema wananchi wa Songea wana imani kubwa na serikali, hata hivyo bado wana shida kubwa ya soko kwa ajili ya mazao yao jambo linalowarudisha nyuma kiuchumi licha ya juhudi kubwa wanazofanya mwaka hadi mwaka.Alisema licha ya serikali kupanga bei ya Sh 500 kwa kilo moja, bado bei hiyo inawanufaisha zaidi mawakala wanaotumia nafasi hiyo kwenda mashambani kununua mahindi kwa bei ndogo ya Sh 200 na kuiuzia serikali kwa bei kubwa na kuwaacha wakulima wakipata hasara.Mbali na hilo aliiomba serikali kuangalia upya utaratibu wa kugawa magunia ya kununulia mahindi kwa mawakala, kwani hauwasaidii wakulima kwa vile magunia hayo yanatolewa kwa watu wenye uwezo wa kifedha au wenye majina makubwa na kusababisha kero kubwa kwa wakulima wa mahindi.Gama aliishauri serikali kugawa magunia kwa wakulima badala ya kuwapa mawakala ambao wanatumia nafasi hiyo kuwanyonya wakulima kwa kwenda vijijini kununua mazao ikiwemo mpunga na mazao mengine ya biashara kwa bei ambayo inamkandamiza mkulima. | 5 |
Kampeni maalum ya uchangiaji kwa klabu ya Yanga iliyobatizwa jina la ‘Kubwa Kuliko’ itazinduliwa rasmi Jumamosi wiki hii katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Upanga jijini Dar es Salaam na wanachama pamoja na viongozi wa Yanga. Hii ni takribani kampeni kubwa ya tatu ya uchangiaji ambapo kwa mara ya kwanza zoezi hili lilizinduliwa jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi, wadau, wafanyabiashara na wanasiasa. Akizungumza na wanahabari leo, Katibu wa Kamati ya Hamasa ya Yanga, Deo Muta amesema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika litaanza saa nne asubuhi hadi saa kumi kamili jioni. Amesema kuwa, tamasha hilo linakwenda kuibadilisha Yanga na kutengeneza historia ndani ya timu hiyo katika kuhakikisha wanafikia malengo yao ya kujiendesha. “Wadau mbalimbali tumewaalika katika tamasha hili kubwa la kihistoria la Kubwa Kuliko ambalo litafanyika kwa siku nzima ya Jumamosi hii wakiwemo wasanii wa Bongo Muvi na Bongo Fleva, wachezaji wa zamani, wanachama na mashabiki. “Tamasha litakuwa ‘live’ likirushwa na kituo cha Televisheni cha Azam TV, pia kwa wale watakaokuwa mbali na TV, tumewarahishia kwa kuweza kuangalia kwa njia ya simu au ‘laptop’ kwa kutumia mfumo wa online wa ‘Pay Per View,”amesema Muta.
| 4 |
MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amezitaka taasisi na wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi, kuongeza jitahada za kuzuia maambukizi mapya kuongezeka.Ametoa agizo hilo katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Baraza la Idd Wilaya ya Tunduru.Akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu huyo wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Juma Homera alisema takwimu zinaonyesha Ruvuma ina kiwango cha maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) cha asilimia 5.6 zaidi ya kile cha Taifa cha asilimia 4.7 kwa mwaka 2016/17.“Takwimu hizi ingawa zinaonekana kushuka kwa kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 7 mwaka 2011/12 bado kunahitajika nguvu na mikakati mipya ya kushusha zaidi kiwango cha maambukizi ya VVU,” alieleza.Ili kuhakikisha maambukizi mapya yanapungua Mndeme alisisitiza mkakati wa upimaji wa hiari wa VVU uimarishwe kwenye wilaya zote tano.Aliongeza kusema ni wakati sasa kuhakikisha watu wote wanaokutwa na VVU wanaanzishiwa tiba mara moja.Mkuu wa wilaya Homera aliishukuru serikali ya awamu ya Tano kwa kuongeza bajeti ya dawa hadi kufikia Sh bilioni1.3 kwa mkoa wa Ruvuma kufikia mwezi Juni 2018 ikilinganishwa na Sh milioni 297.5 zilizotolewa mwaka 2016/2017 kwenda Bohari Kuu ya Dawa (MSD).Mafanikio haya alisema yamesaidia wananchi wengi wa mkoa wa Ruvuma kuwa na uhakika wa matibabu hivyo kuongeza jitihada za kupunguza kasi ya maambukizi ya VVU.Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dk Magdalena Zenda alisema katika kipindi cha Januari hadi Oktoba 2018 jumla ya wananchi 456,777 walipimwa hali zao za maambukizi.Kati yao waliogundulika na maambukizi ni 8,494 ambapo wanaume walikuwa (3,764) na wanawake (4,730).Dk Zenda aliongeza kusema hadi kufikia mwezi Oktoba 2018 Mkoa umefanikiwa kusajili na kuanzisha dawa za kufubaza Virusi (ARV) kwa WAVIU 63,671 tangu huduma hizi zianze mwaka 2004."Kati yao wanaotumia dawa hadi sasa ni 42,056, wanaume ni (14,336) na wanawake (27,720) wanaendelea kupata huduma katika kliniki za tiba na matunzo (CTC) kote mkoani " amesema Dk Zenda.Alitaja changamoto kubwa ni idadi ya wanaotumia ARV wapatao 14,899 kuhamia vituo vingine nje ya mkoa na 11,368 ni wa VVU waliopoteza ufuasi.Katika kipindi cha mwaka 2004 hadi sasa mkoa umekuwa na vifo vitokanavyo na ukimwi 7,168 .Mkoa wa Ruvuma wenye watu takribani 1,449,830 kwa sensa ya mwaka 2012 una vituo vya kutolea huduma za afya 314.Kati yake hospitali zipo (11),vituo vya afya (32) na zahanati (271) hii inafanya huduma za upimaji na matibabu ya VVU kupatikana karibu maeneo yote. Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi mwaka huu 2018 inasema Pima,Jitambue,Ishi. | 3 |
JOHANES RESPICHIUS -DAR ES SALAAM WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema serikali itanunua dawa zinazotengenezwa na wawekezaji wa hapa nchini kwa kuzingatia ubora, usalama na ufanisi. Waziri Mwalimu alitoa masharti hayo jana kwenye hafla ya uzinduzi wa Maabara zinazohamishika uliofanyika kwenye ofisi za Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Dar es Salaam. Alisema baada ya Serikali kuhimiza ujenzi wa viwanda nchini itaanza kununua dawa zinazotengenezwa na viwanda vya ndani lakini kwa wekezaji waliotimiza vigezo. Waziri Mwalimu alisema uzinduzi wa maabara hizo ni moja ya jitihada zinazofanywa na serikali kuondoa bidhaa na dawa bandia ili kuokoa maisha ya raia wake “TFDA imeendeleza mpango mahsusi wa uchunguzi wa awali wa dawa ulionza 2002 katika baadhi ya hospitali za mikoa na vituo vya forodha kwa dawa muhimu za kifua kikuu, dawa za kufubaza virusi vya ukimwi (ARVs) na viua sumu (antibiocs). “Hatua hii ya kununua maabara zinazohamishika 10 na kufikia 25 kote nchini inalenga kuimarisha nguvu katika kudhibiti ubora na usalama wa dawa zinazoingia na zilizoko sokoni. “Na niweke wazi kwamba Serikali haitanunua dawa za ndani ambazo hazikidhi vigezo,” alisema Mwalimu. Aidha Waziri Mwalimu aliitaka TFDA kutowaone aibu na kuwaogopa wawekezaji ambao wataleta dawa bandia bali iwachukulie hatua stahiki bila kujali gharama za mzigo wenyewe. “Wawekezaji walete dawa zenye ubora unaotakiwa hivyo TFDA hata mtu akileta mzigo wa bei ya juu kiasi gani kama hauna ubora msimwonee aibu. “Lakini pia TFDA msikwamishe wawekezaji bali muwe sehemu ya kuwezesha ufikiaji wa uchumi wa viwanda nchini,” alisema Mwalimu. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, alisema maabara hizo 10 zimegharimu Sh milioni 100 na kwamba hivi sasa maabara hizo zimefikia 25 kutoka 15 mwaka 2012/13. Alisema maabara hizo zitapelekwa katika ofisi za kanda tatu za Tabora (Magharibi), Mbeya (Nyanda za juu Kusini) na Mtwara (Kusini) na vituo vya forodha Namanga, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa (KIA), Sirari na Mutukula na katika Bandari ya Dar es Salaam na kwamba maabara nyingine mbili zitapelekwa katika mikoa ya Geita na Katavi. “Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya maabara hizo, uwezo wa kubaini dawa duni na bandia umeongezeka na imewezesha idadi ya dawa duni kushuka kutoka asilimia 3.7 2005 hadi chini ya asilimia 1 mwaka 2017,” alisema. Alisema TFDA ilimebaini dawa bandia zilizodaiwa kuwa na viambata vya Ampicillin, Erythromycin, Quinine Sulphate, Metronidazole na dawa ya mseto ya Metakelfin. | 0 |
MIONGONI mwa changamoto kubwa zinazokwamisha juhudi za wakulima kujiletea maendeleo hasa baada ya kuvuna mazao yaokatika nchi mbalimbali za Afrika ikiwamo Tanzania, ni kuwapo kwa uharibifu wa mazao wakiwemo dumuzi na fukuzi.Profesa Mshiriki katika Kituo cha Udhibiti wa Viumbe Hai Waharibifu, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), ambaye pia ni Mkuu wa Mradi katika Kituo Mahiri cha Mashariki na Kusini mwa Afrika kinachohusika na utafiti wa panya na matumizi yake katika unusaji, Apia Massawe anasema panya pia wamekuwa waharibifu na wanaosumbua wakulima.Profesa Massawe ambaye pia ni Mkuu wa Mradi unaofadhiliwa na serikali wa kupunguza matatizo ya wadudu katika maghala na nyumbani kwa wakulima wadogo wadogo, anasema wapo pia panya wanaokula mazao yakiwamo mahindi na hata kusababisha usumbufu mwingine kwa binadamu na wanyama.Mbobevu huyo katika utafiti wa panya ambaye amekuwa akifanya utafiti kuhakikisha hawaleti madhara kwa wakulima nyumbani na shambani, Mradi wa Hifadhi Bora wa Mazao kwa kutumia mifuko maalumu unaofadhiliwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) ulianza mwaka 2012 na ulitarajiwa kuisha mwaka jana, lakini umeongezewa muda mpaka Machi mwakani. Katika mradi huo, Costech imetoa Sh milioni 89 kuwezesha watafiti hao wa SUA.Anasema utafiti huo umelenga kuangalia matumizi bora ya uhifadhi wa mifuko ya nafaka kwa wakulima wadogo. “Kama watafiti, tumehangaika kutafuta njia nyingi za kusaidia wakulima, ikiwa ni pamoja na kuweka kwenye vihenge ili kuzuia panya, lakini bado dumuzi na fukuzi wamekuwa wakisumbua,” anasema.Anasema ili kukabiliana na hali hiyo, wakulima wengi wamekuwa wakitumia viuatilifu kuua wadudu na mimea mbalimbali, lakini katika kuhifadhi bado ni tatizo. “Hizi dawa athari zake zimekuwa kubwa kwa wakulima.Unakuta mtu anasaga unga wa dona bila kuosha anakula anakuwa amekula sumu na madhara yake ni makubwa… Tukaangalia ni njia ipi itasaidia wakulima wengi kwani wapo waliojitahidi kutumia hata mapipa kuhifadhi lakini changamoto ipo kwenye nyumba zetu kwani mkulima ataweka mapipa mangapi ili ahifadhi?” Anahoji Profesa Massawe.Anasema waliona njia bora ni kutumia mifuko ya uhifadhi wa nafaka iliyobuniwa na Chuo Kikuu cha Pado-United State ili kusaidia Afrika Magharibi kuhifadhi mazao ya nafaka. Kwa mujibu wa Profesa Massawe, baada ya kugundua kuna kiwanda kinachotengeneza mifuko hiyo hapa Tanzania lakini wakulima hawana habari kuhusu kiwanda hicho, walijiuliza ni kwanini wakulima hawakitumii, ndipo walipofanya utafiti na kujua sababu.“Tukaona tunahitaji kufanyia utafiti ili tuone hiyo mifuko inafanyaje kazi ili wakulima waweze kuitumia,” anasema. Kama watafiti walipata fedha za utafiti kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) kisha wakaanza utafiti ulioeleta matokeo mazuri. Mradi huo umefanyika Berega wilayani Gairo na katika Kijiji cha Mgugu mkoani Morogoro. Anasema: “Wakulima watanufaika sana kwa kutumia mifuko hii.Unapotumia na kufanya vizuri wadudu wanakufa na hakuna mdudu atakayeingia na kuharibu mazao ndani ya mfuko huo. Hata panya hana uwezo wa kutoboa mfuko huu kwa sababu hutoboa kitu baada ya kunusa, lakini ukihifadhi nafaka zako vizuri ndani ya mifuko mitatu hawezi kutoboa.”“Mkulima atakuwa na uhakika wa kupata chakula mwaka mzima, kama anataka kuuza, atauza wakati ambao bei inakuwa nzuri tofauti na wakati kabla ya kuanza kutumia mifuko hiyo walipouza ili nafaka zao zisishambuliwe na wadudu,” anasema.Profesa Massawe anasema kwa kuwa wakulima walikuwa hawana uhakika wa kuuza mazao yao, waliuza mapema kwa bei ndogo, lakini watauza kwa bei nzuri na hata matumizi ya mifuko hiyo yatapunguza utumiaji wa viuatilifu. Mwitikio ukoje? Baada ya utafiti wa mwanzo na kuanza kutangaza mifuko hiyo, mwitikio umekuwa mkubwa, ingawa upatikanaji wa mifuko hiyo ulikuwa ni mgumu kidogo.Profesa Massawe anasema, wao kama watafiti wa SUA wakiwa kiungo kati ya kiwanda na wakulima ili kuwezesha wakulima waipate kwa urahisi na hivi sasa wengi wao wanaitumia. Upatikanaji wa mifuko ulivyo Profesa huyo anasema wamezungumza na watu wa viwandani wa Pee pee Tanzania Limited na A to Z kama wanaweza kuzalisha kwa wingi ili wawauzie wakulima, lakini pia yapo maduka ya pembejeo yanayouza mifuko hiyo japo ni ghali kidogo kwani mmoja unauzwa kati ya Sh 5,000 na Sh 6,000. “Tunajaribu kuzungumza na viwanda kama wataweza kuzalisha kwa bei ya chini ili wakulima wote waweze kuitumia mifuko hiyo,” anasema.Anaelezea faida za mifuko hiyo mbali na kuhifadhi nafaka zisishambuliwe na wadudu, kuwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kutumika hata mara tatu bila kuharibika. “Kwa kutumia hii mifuko hii, wakulima watakuwa wamepunguza gharama, pia hawatatumia sumu tena na hawatauza mazao yao haraka kwa kuhofia kuharibiwa na wadudu,” anasema.Anasema kama chuo kikuu, wamekuwa wakijitahidi kutoa elimu kuhusu matumizi ya mifuko hiyo kwa njia mbalimbali ili jamii iweze kuitumia kwa ufasaha. Mtaalamu huyo anasisitiza kuwa, wataendelea kutoa mafunzo kwa mabwana shamba nchi nzima, ikiwa ni pamoja na kutoa vipeperushi vya kutosha ili ifikapo Machi mwakani kabla mradi huo, Watanzania wengi wawe wamepata elimu.Anasema baada ya utafiti huo kufanya vizuri, elimu kuhusu faida na utumiaji wa njia hiyo ni muhimu iwafikie watu wengi zaidi. Mwenyekiti wa Kijiji cha Berege, David Aron anasema wamenufaika na mradi huo kwa sababu hivi sasa hawaweki dawa kwenye nafaka zao, na badala yake wanahifadhi kwenye mifuko hiyo. “Kwenye mfuko mmoja unaweka mahindi debe sita, tofauti na viroba vya kawaida ambavyo ukiweka mahindi au nafaka nyingine inabanguliwa,” anasema.Mkulima kutoka Kijiji cha Berege, Jones Ngiga, anasema analima mahindi na mbaazi eka tatu na amepata magunia 30 anayohifadhi kwenye mifuko hiyo. Kwa maelezo yake anasema, amekuwa mhamasishaji kwa wakulima wenzake kuhusu kutumia mifuko hiyo kuhifadhi nafaka baada ya kuona mafanikio yake.Mkulima mwingine Betina Chibwaya anayeishi katika Mtaa wa Mlingoti A, kijiji cha Berege anasema ni mkulima wa mahindi na kipindi hiki mazao hayo hayana bei, hivyo ili hataki kuyauza kwa hasara, hivyo ameyahifadhi kwenye mifuko hiyo hadi bei itakapokuwa nzuri.Mkurugenzi Kituo cha Kudhibiti Viumbe Hai Waharibifu chuoni hapo, Dk Ladislaus Mnyone anasema wamekuwa na miradi miwili kutoka Costech, mmoja ukiwa huu wa kuhifadhi mahindi yasibanguliwe na wadudu waharibifu, na mwingine ni wa kutumia mkojo wa paka kudhibiti panya waharibifu.Anasema kumekuwa na matumizi makubwa ya kemikali katika nafaka hivyo kutumia mifuko hiyo, kutapunguza matumizi hayo ya dawa. Anasema anashukuru kituo chake kupata fursa ya kufanya utafiti wenye matokeo chanya kwa jamii, lakini pia ni vipaumbele vya taifa, ikiwa ni pamoja na watafiti kufanya kazi na watu wengine. | 3 |
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40) na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu. | 5 |
Taifa Stars wamemaliza safari yao ya Afcon kwa kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Mbweha wa Kaskazini Algeria, katika mchezo wa kukamilisha ratiba wa Kundi C uliofanyika kwenye Uwanja wa Al-Salam uliopo jijini Cairo nchini Misri. Mshambulizi wa Napoli Adam Ounas ndiye alikuwa mwiba kwa Stars baada ya kufungwa mabao mawili na kutoa pasi moja ya goli katika mchezo huo, ukiwa ni mchezo wake wa kwanza katika michuano ya AFCON. Straika wa Leicester City Islam Slimani ndiyo alifungua ukurasa wa mabao kwa Algeria kufuatia pasi nzuri kutoka kwa Adam Ounas dakika ya 35. Algeria ambao wamemaliza kama vinara wa Kundi C tayari walikuwa wameshafuzu baada ya kushinda michezo yao miwili ya awali. Watakutana na timu inakayopata nafasi ya mshindi wa tatu bora katika kundi lolote kwenye hatua inayofuata. Wakiwa tayari wamefuzu kabla ya mchezo dhidi ya Tanzania, kocha wa Algeria Djamel Belmadi alifanya mabadiliko tisa ya kikosi chake kilichoanza katika mechi mbili za awali na kumuanzisha Islam Sliman badala ya straika wa Al Sadd ambaye yuko kwenye kiwango bora kwa sasa Baghdad Bounedjah Na Slimani aliitumia nafasi hiyo kufunga bo lake la 27 katika timu ya taifa ndani ya michezo 61 aliyocheza Ounas aliongeza magoli mawili mnao dakika za 39 na 45 na kukamilisha idadi ya mabao matatu kwa bila kwa Mbweha hao dhidi ya Tanzania. Kwa upande wa Taifa Stars, almanusura wapate goli la kufutia machozi kutoka kwa straika anayekipiga Blackpool Adi Yussuf lakini mpira wake wa kichwwa uligonga mwamba. Kwa matokeo hayo sasa, Tanzania imemaliza ikiwa mkiano kabisa mwa Kundi C bila alama yoyote na kuwa mzigo wa kufungwa wa magoli. Katika mchezo mwingine wa KUNDI C, Kenya wamepokea kipigo kizito cha mabao 3-0 kutoka kwa Senegal, magoli mawili yakifungwa na mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane na lingine likifungwa na Ismaila Sarr. Katika mchezo huo Mane alikosa penati ambayo kama angefunga basi pengine angetoka na hattrick. Senegal sasa watachuana na Uganda tarehe 5 mwezi Julai. Kenya inaweza ikafuzu kama timu ya tatu bora ikitegemea matokeo katika mechi ya mwisho katika Kundi E and F. Hata hivyo matokeo ya Jumatatu yanamaanisha kwamba DR Congo inaweza kufuzu kutoka kundi A ikiwa na goli moja zaidi. | 4 |
Hayo yalibainishwa na Meneja wa Kituo cha Kilimo cha Laela wilayani Sumbawanga, Ray Mtetewaunga alipokuwa akizungumza na gazeti hili kando ya mdahalo wa wadau wa kilimo uliofanyika mjini hapa hivi karibuni.“Kutokana na wakulima mkoani hapa kukosa soko la uhakika la kuuzia mazao yao ya chakula hususan mahindi wamekuwa wakilazimika katika misimu kadhaa ya mavuno kuuza mahindi yao kwa walanguzi kwa bei ya kutupwa kati ya Sh 10,000 na 25,000.Msimu huu wa kilimo ambapo mavuno ya mahindi yamekuwa hafifu bei imepanda kiasi kidogo ambapo wakulima wanauza kwa walanguzi gunia moja lenye uzito wa kilo 100 kwa bei ya rejareja ya Sh 30,000” alisema.Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na Viwanda (TCCIA) mkoani Rukwa, John Msabaha alisema kuwa masoko ya mahindi ndani na nje ya nchi sio tatizo tena isipokuwa mahindi kutoka mkoa wa Rukwa hayauziki katika masoko hayo kutokana na kutokuwa na ubora unaohitajika.Pieta Mawazo mkulima kutoka kijiji cha Kavifuti wilayani Sumbawanga akichangia katika mdahalo huo, alieleza kuwa baadhi ya wakulima ambao si waaminifu wamekuwa wakichanganya ufuta na mchanga hivyo kupoteza ubora wake katika masoko ya ushindani.Ofisa Kilimo wa Hamashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Kwileluye Habona amebainisha chagamoto za uzalishaji na uuzaji wa zao la mahindi akisema kuwa wakulima wanashindwa kulima maeneo makubwa kutokana na ukosefu wa soko la uhakika ambapo husababisha kuuza mahindi kwa bei ya chini ukilinganisha na gharama za uzalishaji.“Kwa mfano gharama ya kuzalisha gunia moja la mahindi lenye uzito wa kilo 100 ni Sh 39,615 kwa wastani , lakini mkulima amekuwa akiuza gunia hilo kati ya Sh 15,000 hadi 20,000 kwa walanguzi pale ambapo Serikali kupitia Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) Kanda ya Sumbawanga wanapokuwa haijanunua,”alieleza Kwileluye.Takwimu za ulinganifu wa kiasi cha mahindi kilichouzwa kwenye masoko rasmi na yasiyo rasmi kwa misimu miwili ya mwaka 2013-14 na 2014 -15 inaonesha kuwa wakulima wilayani Sumbawanga walivuna tani 115,412.9 za mahindi ambapo NFRA Kanda ya Sumbawanga ilinunua tani 9,441.76 sawa na asilimia 8.18 ya ziada ya mahindi iliyozalishwa kwa msimu huo .Katika msimu huo wa mavuno tani 105,971.14 ziliuzwa nje ya mfumo usio rasmi kwa bei ya kutupwa.Katika msimu wa 2014-15 wakulima walizalisha ziada ya tani 121,627.9 za mahindi ambapo NFRA ilinunua tani 14, 241.9 za mahindi na tani 107,385.9 zilikuzwa katika masoko yasiyo rasmi. | 5 |
Na CHRISTIAN BWAYA KWA muda mrefu, utamaduni wa kubeba watoto mgongoni umekuwa sehemu ya malezi katika jamii nyingi za Kiafrika. Tangu mtoto anapozaliwa, wanafamilia hupokezana kumshika na kumbeba kama namna ya kuonesha furaha yao. Ni nadra mtoto mchanga kubaki mwenyewe kitandani isipokuwa katika nyakati fulani fulani. Sambamba na kubebwa mgongoni, mtoto huyu hulala kitanda kimoja na wazazi wake hadi hapo atakapofikia umri wa kuhamia chumba kingine aweze kulala na wenzake. Jamii nyingine nje ya Bara la Afrika zinapata shida kuelewa desturi hii. Kwao ni rahisi kufikiri kuwa kumweka mtoto mgongoni ni aina fulani ya ukatili na kumkosea mtoto haki ya kuwa huru. Katika jamii hizo, watoto huzoezwa maisha ya upekee tangu wanapokuwa wadogo. Pamoja na tofauti hiyo ya kiutamaduni, mambo yameanza kubadilika kwa kasi hapa kwetu. Imeanza kuwa kawaida kwa mfano, kwa wazazi kuwaandalia watoto vitanda vyao tangu wanapozaliwa. Watoto wameanza kulala peke yao. Ule utaratibu wa mtoto kubebwa kifuani au mgongoni mwa mzazi wake pia umeanza kupotea. Badala yake, wazazi huwaweka watoto katika vifaa maalumu wanapokuwa matembezini sambamba na kuwalaza kwenye vitanda vya kujitegemea. Zipo sababu nyingi zinazoweza kueleza kwanini mambo yamebadilika. Kwa mfano, kuna suala la mwingiliano wa utamaduni baina ya jamii mbalimbali. Hivi sasa, mathalani, ni rahisi kwa mzazi wa Simiyu kujua mtindo wa maisha ya wazazi wa barani Ulaya na hivyo kubadili kabisa namna anavyoishi. Lakini pia, mwingiliano huu unapokwenda sambamba na kuimarika kwa uwezo wa kiuchumi, inakuwa rahisi kwa wazazi kubadili namna yao ya maisha. Wazazi wenye kipato cha kati, kwa mfano, wanaweza kutengeneza kitanda maalumu kwa ajili ya mtoto mchanga kwa sababu wanao uwezo huo. Pamoja na mabadiliko haya, ni muhimu kuelewa kuwa utamaduni huu wa kubeba watoto ni suala la kimaumbile kuliko lilivyo kiutamaduni. Hata katika makundi ya wanyama wengine mbali na mwanadamu, kubeba watoto ni kawaida. Kisayansi, watoto huzaliwa na hitaji ndani yao la kuunganishwa kimahusiano na watu wengine. Wanazaliwa na njaa ya kutengeneza ukaribu na watu. Katika umri pungufu ya miaka mitatu, watafiti wanasema mtoto anahitaji ukaribu mkubwa wa kimwili na kihisia na wazazi wake. Mzazi, anahitajika kufanya juhudi za kuwa karibu na mwanawe ili kujenga uhusiano huo. Kwa ushahidi huo, mantiki ya desturi ya kubeba na kukumbatia watoto, ambayo kwa Afrika ni sehemu ya maisha ya kila siku, inapata nguvu. Tunahitaji kurekebisha makosa yanayoanza kufanyika katika jamii yetu. Tunahitaji kurudia desturi ya kubeba, kulala na kuwakumbatia watoto wachanga. Watafiti wengi wa makuzi wamepata ushahidi wa kisayansi kuwa watoto wachanga wanaobebwa mara kwa mara hujenga ukaribu wa kihisia na wazazi na hivyo huwa na nafsi zilizotulia ukilinganisha na watoto wasiobebwa. Ndio kusema, pamoja na mabadiliko ya kijamii yanayoendelea, ni vyema kuendeleza desturi ya kubeba watoto kama ilivyokuwa hapo zamani. Tunahitaji kurudia desturi ya kulala na watoto wachanga. Kwa kufanya hivyo, tunajenga misingi imara ya kuwa karibu nao wangali wadogo. Madai kwamba kulala na watoto wachanga ni kuwaambukiza magonjwa, hayana nguvu ya kuondoa mantiki ya desturi hii. Tujenge mazoea ya kuwakumbatia mtoto kila inapowezekana. Kuwakumbatia kunawahakikishia kuwa wako salama. Christian Bwaya ni mhadhiri wa saikolojia na unasihi, Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU). Simu: 0754 870 815 | 0 |
MADALALI wa Mahakama na Wasambazaji nyaraka za mahakama wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia misingi ya kazi yao ili kujenga taswira nzuri kwa mahakama nchini na mahakama hiyo haitasita kuchukua hatua za ukiukwaji wa maadili kwa wale watakaobainika.Jaji Kiongozi wa Mahakama kuu ya Tanzania, Dk Eliezer Feleshi ameyasema hayo mjini Morogoro wakati akifunga mkutano wa wadau juu ya kuongeza idadi ya madalali wa mahakama na wasambazaji nyaraka za mahakama nchini.Amesema tasnia ya madalali wa mahakama na wasambazaji nyaraka za mahakama inaendelea kukua kutokana na kupatikana vijana wengi wasomi tofauti na mwanzo, hivyo ni wajibu wao kuendelea kujenga taswira nzuri kwa mahakama na jamii.Pamoja na hayo alisema mahakama itaendelea kufungua milango kwa madalali wa mahakama na wasambazaji nyaraka za mahakama na itendelea kuwalinda wale wenye tabia nzuri za utendaji wa kazi zao.Hivyo aliwaonya wasifanye makubaliano batili na watumishi wa mahakama hususani mahakimu katika kutekeleza majukumu yao, bali wafanye kazi zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.Jaji Kiongozi wa mahakama kuu ya Tanzania, Dk Feleshi ametumia fursa hiyo kuwaomba viongozi wa serikali ngazi za mikoa na wilaya kutowazuia madalali wa mahakama wakati wakitekeleza majukumu yao, kwani kwa kufanya hivyo wanatenda kosa.Awali, Naibu Msajili Masijala Kuu Mahakama Kuu ya Tanzania, Sharmilla Sarwatt aliwasilisha maazimio 13 ya wadau hao ikiwemo kuanzisha Chama cha Madalali wa Mahakama nchini kitakachokuwa chombo kuinganisha na Mahakama katika utendaji wao wa kila siku.Sarwatt alisema miongoni mwa maazimio hayo ni pendekezo kwa madalali wa mahakama na wasambazaji nyaraka za mahakama kupewa vitambulisho na kuvaa sare maalumu kama ilivyo kwa watumishi wa mahakama, ili wafahamike vyema na hilo litasaidia kuwabaini madalali vishoka. | 3 |
BAADA ya Manchester United kutolewa kwenye michuano
ya Kombe la FA dhidi ya Wolves, kocha wa timu hiyo, Ole Gunnar Solskjaer, amewajia
juu wachezaji wake kwa kitendo cha kucheza mfumo wa Jose Mourinho. Manchester United ilikubali kichapo cha mabao 2-1
dhidi ya Wolves kwenye hatua ya robo fainali, ambayo ilipigwa kwenye uwanja wa
Molineux na kuondolewa kwenye michuano hiyo. Kwa mujibu wa The Sun, Solskjaer aliwashangaa
wachezaji wake katika dakika 45 za kipindi cha kwanza na kuwataka wabadilike
dakika za mwisho kwa ajili ya kupata matokeo, lakini walishindwa kufanya hivyo
na kujikuta wakitolewa. Hata hivyo, kocha huyo amewataka wachezaji wake
kila mmoja kuhakisha anaeleza kwa nini walicheza chini ya kiwango. Bila kujali Man United imesalia kwenye michuano mikubwa
ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, anaamini walikuwa na nafasi kubwa ya kutwaa Kombe
hilo la FA. “Tumerudi hatua nyingi nyuma, naweza kusema kwamba
United wameonesha kiwango cha chini sana tangu nimewasili hapa. Tulicheza
vizuri katika mchezo dhidi ya Arsenal, lakini hatukupata kile tulichokitarajia. “Nadhani wachezaji wangu walijisahau na kucheza
mfumo ambao walikuwa wanautumia na kocha Jose Mourinho, lazima wabadilike na
bila kufanya hivyo tunaweza kujikuta tunaelekea pabaya. “Najua hauwezi kuwa kwenye kiwacho cha hali ya juu
katika kila mchezo msimu wote, kuna wakati unakutana na changamoto mbalimbali,”
alisema kocha huyo. Kocha huyo aliongeza kwa kuwatoa wasiwasi mashabiki
wa timu hiyo kuelekea michezo ijayo huku akidai wanaelekeza nguvu zao huko kwa
ajili ya matokeo. Mchezo unaofuata kwa Manchester United ni dhidi ya Watford
mwishoni mwa mwezi huu, baada ya kupisha michezo ya Kimataifa wiki hii. United
inashika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 58, baada ya
kucheza michezo 30. Wakati huo Liverpool wakiwa vinara kwa pointi 76,
wakifuatiwa na Man City wenye pointi 74, lakini Liverpool wanaongoza kwa mchezo
mmoja. | 4 |
RAIS John Magufuli anafanya ziara ya siku tano mkoani Dodoma, ambapo ataweka mawe ya msingi katika miradi mitano ya maendeleo ya kiuchumi na kuzungumza na wananchi katika mikutano mbalimbali ya hadhara.Katika ziara hiyo inayoanza Novemba 21, Rais Magufuli ataanza kwa kuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) yatakayofanyika kwenye Ukumbi wa Chimwaga jijini hapa.Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu ziara hiyo jijini hapa jana, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge, alisema siku ya pili ya ziara yake, Rais atatembelea na kuweka jiwe ya msingi kwenye mradi wa Hospitali ya Uhuru wilayani ya Chamwino.“Pia ataweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa nyumba 118 za askari polisi katika eneo la FFU Nzuguni na Medeli East. Pia ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa stendi kuu ya mabasi na soko kuu eneo la Nzuguni,” alisema.Dk Mahenge alisema baada ya Rais Magufuli kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo, atafanya mkutano wa hadhara katika eneo la stendi ya mabasi Nzuguni jijini Dodoma na kuzungumza na wananchi.Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Jumatatu, Novemba 25, mwaka huu, baada ya Novemba 24 kushiriki katika kupiga kura kijijini kwake Chamwino alikojiandikisha ili kuchagua viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika nchini kote siku hiyo.Siku hiyo pia ataweka jiwe la msingi kwenye miradi ya ujenzi wa makao makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikombo, ujenzi wa ofisi ya makao makuu ya idara ya uhamiaji na ujenzi wa jengo la makandarasi katika eneo la National Capital City jijini hapa.Dk Mahenge amewataka wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika mikutano ya hadhara ya Rais Magufuli ili kusikiliza maelekezo ya kiongozi huyo kuhusu miradi hiyo inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali mkoani humo.Alisema miradi hiyo mitano itakayowekwa mawe ya msingi na Rais Magufuli ni awamu ya kwanza ya uwekaji mawe ya msingi kati ya miradi 26 ya maendeleo iliyoombwa kuwekewa mawe ya msingi. | 3 |
|Sarah Moses, Dodoma Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewatoa nje Makamanda zaidi ya 30 kwa kosa la kutaja Jeshi la Zimamoto bila kumalizia ‘na Uokoaji’ ambapo amesema hilo jeshi lao halitambui. Hali hiyo imejitokeza leo Alhamisi Agozti 30, jijini Dodoma kwenye ufunguzi wa kikao cha mwaka cha Makamanda wa Zimamoto na Uokoaji ambapo amesema makamanda hao wamekuwa wakifanya kazi kwa mazoea. “Mimi nalijua Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wale wote ambao walijitambulisha bila kumalizia na uokoaji watoke nje. “Nisikilizeni kwa makini makamanda ambao nimewaita majina yenu simameni na ambao hamjasikia nikitaja majina yenu tokeni nje kwani hilo jeshi lenu mlilolitaja silitambui hivyo kikao hiki hakiwahusu. “Haiwezekani ofisa mzima unasimama unajitambulisha kuwa unatoka Jeshi la Zimamoto, kwa hiyo kazi yenu nyinyi ni kuzima moto tu na siyo pamoja na uokoaji,” amesema. Waziri Lugola alisema amefanya hivyo kwa kuwa anataka jeshi hilo lijitambue kuwa ni jeshi lenye majukumu hayo kwani lipo na lilianzishwa kwa mujibu wa sheria kuwa ni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Hata hivyo, Lugola baada ya kuwatoa nje makamanda hao aliwaruhusu kuingia kushiriki kikao hicho wakiwa kama wageni waalikwa na si wahusika wa kikao hicho. | 0 |
Ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na wenye viwanda na wajasiriamali mbalimbali, wakati wa kuadhimisha Siku ya Viwanda Afrika iliyoadhimishwa katika viwanja wa maonesho wa Mwalimu J.K. Nyerere.Alisema sekta ya viwanda vidogo vina nafasi kubwa katika kukuza ajira, kuondoa umasikini na kuongeza pato la mwananchi mmoja mmoja na pato hilo limekuwa likikua hatua kwa hatua. “Hivi sasa sekta hii ina viwanda vidogo zaidi ya milioni tatu vinavyoajiri zaidi ya Watanzania milioni 5.2.Mchango wake katika pato la taifa ni asilimia 27 na kwenye ajira ni asilimia 23.4 ya nguvu kazi yote nchini,” alisema.Alisema msukumo mkubwa uliowekwa na Serikali ya Awamu ya Nne katika kuendeleza viwanda, ni pamoja na uanzishwaji na uendelezaji wa maeneo ya fursa huru za uwekezaji kama Mamlaka ya Maeneo Huru ya Uzalishaji kwa Mauzo Nje (EPZA) na Maeneo Maalumu ya Uwekezaji (SEZ).“Serikali imechukua hatua za kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika uwekezaji na biashara katika soko la ushindani. Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuipa nguvu ya kisheria EPZA kusimamia uwekezaji wa maeneo ya SEZ. Katika maeneo hayo, wawekezaji wa sekta mbalimbali watazalisha na kuuza bidhaa katika masoko ya ndani na nje ya nchi,” alisema Waziri Mkuu.Kuhusu usimamizi katika uwekezaji, Waziri Mkuu alisema Serikali imeendelea kusimamia uwekezaji katika maeneo maalumu ya uzalishaji ili kuharakisha maendeleo ya viwanda.“Uendelezaji wa maeneo ya EPZ na SEZ ni moja ya mikakati ya kukuza ajira, uwekezaji na uzalishaji viwandani. Mpango huu una maeneo 10 yaliyoonesha mafanikio makubwa yakiwa yameajiri wafanyakazi 27,000.Miradi yote itakapokamilika, inatarajia kuajiri wafanyakazi 273,581,” aliongeza.Alisema katika miaka sita iliyopita, EPZA imeanzisha viwanda 81 katika maeneo mbalimbali nchini ambavyo vimewekeza mtaji wa zaidi ya Dola za Marekani bilioni 1.12 na vimetoa ajira za moja kwa moja 27,000 na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 80,000.Pia mauzo ya nje yamefikia Dola za Marekani milioni 700 na Serikali inaendelea kuimarisha EPZA, ili ichochee ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kupitia maendeleo ya viwanda.Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mku, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda alisema sekta ya viwanda nchini bado inakua kwa kasi ndogo ikilinganishwa na nchi nyingine duniani.“Sekta ya viwanda hapa nchini inakua kwa asilimia tisa wakati China sekta hiyo imekua kwa asilimia 40, Vietnam imekua kwa asilimia 20 na India imefikia asilimia 16,” alisema.Maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) nchini, Emmanuel Kalenzi, Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), Felix Mosha na wawakilishi wa Jumuiya za Kimataifa. | 5 |
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi ambao majina yao hayakuweza kutambulika mara moja, wameuawa na askari wa Jeshi la Polisi wilayani Muheza katika majibizano ya kurushiana risasi.Tukio hilo lililozua hofu lilitokea jana asubuhi katika mtaa wa Ngwaru Kanisani kata ya Kwemkabala, Muheza Mjini wakati majambazi hao wakiwa katika jaribio la kutaka kupora fedha kwa mfanyabiashara maarufu wa mjini Muheza, Jackon Mhufu.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililoteka hisia za wakazi wa mji wa Muheza kwa siku nzima jana. Majambazi hao walifika katika eneo hilo la tukio wakiwa katika gari aina ya Toyota X-Trail lenye namba za usajili T883DJW rangi nyeusi ambapo polisi waliokuwa wameweka mtego walianza kulirushia risasi gari hilo kwenye matairi na kulifanya kushindwa kutembea.Majambazi hao walikuwa katika jaribio la kuvamia nyumba ya mfanyabiashara maarufu huyo kwa lengo la kutaka kupora fedha. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, majambazi hao walianza kurushiana risasi na askari polisi na baada ya kuzidiwa walianza kukimbia huku na kule ndipo wananchi wakatoa ushirikiano na kufanikisha mauaji hayo. “Hawa majambazi walikuwa wanarushiana risasi na polisi ndipo wakauawa...na wananchi walitoa ushirikiano kwa Polisi ambapo waliwadhibiti vilivyo,” alisema Haji Ally.Miili ya majambazi hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali Teule ya Mtakatifu Augustine Muheza kwa ajili ya taratibu nyingine ikiwemo kuwatambua. Hii ni mara ya pili kwa majambazi hao kumvamia mfanyabiashara huyo kwa jaribio la kutaka kupora fedha lakini jeshi la polisi wilayani Muheza walifanikiwa kuwadhibiti. | 3 |
Singida United itakuwa mwenyeji wa Yanga kwenye Uwanja wa Namfua, mchezo unaotabiriwa kuwa mgumu kutokana na makocha wote kuwa bora huku Pluijm akiwa anawafahamu vizuri wapinzani kwani aliwahi kuwafundisha.Katika mechi za mashindano walizokutana, ligi raundi ya kwanza walitoka suluhu na michuano ya Kombe la Mapinduzi walikuwa kundi moja, walitoka sare ya bao 1-1.Mechi hiyo ni ya pili kwa timu hizo kukutana uwanja wa Namfua, ya kwanza ikiwa ya Ligi Kuu ambayo walitoka suluhu. Makocha wote wameonesha ubora kutokana na rekodi zifuatazo:Lwandamina ameiongoza Yanga kushinda michezo 13 kati ya 21 ya ligi, akipata sare saba na kupoteza mchezo mmoja, ikiwa inashika nafasi ya pili kwa pointi 46.Pluijm licha ya kuwahi kutamba kwa mataji wakati akiiongoza Yanga, katika timu yake ya sasa Singida ambayo ni ngeni kwenye ligi, ameshinda michezo tisa kati ya 21, akipata sare tisa, akipoteza michezo minne, wakishika nafasi ya tano kwa pointi 36.Ni makocha bora kwa sababu wakati Pluijm akiwa Yanga iliisaidia mwaka juzi kutinga hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na Lwandamina aliisaidia Zesco kuingia makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.Hivyo, kila mmoja atakuwa anasaka rekodi yake, Pluijm anataka kuvuka hatua hiyo ya robo fainali na kuingia hatua inayofuata na kadhalika, Yanga inataka kuendeleza rekodi yake ya kusonga mbele.Mchezo huo huenda ukawa na presha kubwa hasa kwa Yanga ambayo haina uhakika wa kutetea taji la ligi licha ya kuwa bado wapo kwenye mbio hizo, hivyo wakipoteza dhidi ya Singida watakuwa kwenye wakati mgumu na hatihati ya kutoshiriki michuano ya kimataifa mwakani.Kutokana na umuhimu wa mchezo huo kwa kila mmoja, Yanga imeweka kambi Morogoro na Singida Dodoma kuhakikisha wanawaandaa wachezaji wao vizuri kisaikolijia. | 4 |
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva kutoka katoika lebo ya muziki iliyochini ya diamond Platnumz, WCB Rayavnny amethibitisha kuachana na mama mtoto wake Fahym. Hatua hiyo imekuja kufuatia vuguvugu linaloendelea mitandaoni kwamba wawili hao wameachana na kila mmoja ana hamsini zake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rayvanny ametupia chats za wawili wao akionyesha meseji za Fahyma akimwambia ahesabu kama yeye na mtoto wao (Jaydan) amekufa na kwamba atapambana na hatakosa pesa ya kula. Rayvanny aliweka meseji hizo zikiambatana na majibu yake yaliyosomeka hivi; NIMEKUA NAKUHESHIMU MIAKA YOTE TULIOKUA PAMOJA KUNA MENGI TUMEKOSEANA NA TUMESAMEHEANA NA MOST OF THE TIME UMEKUA UKITAMANI MAISHA AMBAYO KILA SIKU NAKWAMBIA HAYATAKUSAIDIA …. NAKUHESHIMU NA NAISHEMU SANA FAMILIA YANGU …. IKIWA UMEAMUA MWENYEWE KUONDOA I WON’T BLAME YOU ….. STILL LOVE MY FAMILY …NAKUTAKIA MAISHA MEMA 🙏🙏🙏🙏 NIMEKUA NAKUHESHIMU MIAKA YOTE TULIOKUA PAMOJA KUNA MENGI TUMEKOSEANA NA TUMESAMEHEANA NA MOST OF THE TIME UMEKUA UKITAMANI MAISHA AMBAYO KILA SIKU NAKWAMBIA HAYATAKUSAIDIA …. NAKUHESHIMU NA NAISHEMU SANA FAMILIA YANGU …. IKIWA UMEAMUA MWENYEWE KUONDOA I WON'T BLAME YOU ….. STILL LOVE MY FAMILY …NAKUTAKIA MAISHA MEMA 🙏🙏🙏🙏 A post shared by VANNYBOY (@rayvanny) on Nov 23, 2019 at 5:09am PST Mashabiki nao walifunguka na kutoa maoni yao huku baadhi wakionyesha kumpa pole Rayvanny na wengine wakisema hayo ni mambo ya kiki tu. | 1 |
DORTMUND, UJERUMANI SHABIKI wa klabu ya Borussia Dortmund, amefariki dunia juzi wakati wa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mainz 05, kwenye Uwanja wa Signal Park. Katika mchezo huo, Dortmund ilifanikiwa kushinda mabao 2-0 ambayo yalifungwa na Marco Reus pamoja na mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Manchester United, Shinji Kagawa, lakini hakushangilia kutokana na kifo cha shabiki huyo. Shabiki huyo alipoteza maisha katika dakika ya 30 ya mchezo huo baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo. Taarifa ya kifo cha shabiki huyo zilienea ndani ya dakika 15 ambapo idadi kubwa ya mashabiki walipata taarifa hadi kufikia wakati wa mapumziko. Kipindi cha pili kilipoanza wachezaji wote pamoja na mashabiki walisimama kwa ajili ya kufanya maombi ya kifo hicho. Hata hivyo, shabiki mwingine alikimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu baada ya kupoteza fahamu kutokana na mshtuko wa moyo, lakini hali yake inadaiwa kuendelea vizuri. Rais wa klabu ya Dortmund, Reinhard Rauball, kupitia mtandao wa klabu hiyo ametuma salamu za pole kwa familia ya marehemu na mashabiki wote kwa ujumla. | 4 |
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imefungua tena udahili kwa awamu ya nne ya maombi ya masomo kwa mwaka 2018/19 kwa vyuo vya elimu ya juu nchini kutoa nafasi kwa wanafunzi wenye sifa waliokosa nafasi hizo katika awamu zilizopita.Imevitaka vyuo na taasisi za elimu ya juu nchini kutangaza programu ambazo zina nafasi na idadi ya nafasi zilizopo ili waombaji waweze kutuma maombi hayo yaliyofunguliwa kuanzia jana hadi Oktoba 20, mwaka huu.Tume hiyo kupitia taarifa yake iliyotolewa juzi, imewataka waombaji kuhakikisha wanazingatia Kitabu cha Mwongozo wa Udahili sambamba na kuangalia ufaulu wa masomo yao.Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, baadhi ya waombaji walikosa nafasi kutokana na kuomba fani ambazo hazina uwiano na ufaulu wa masomo yaliyosoma.Akizungumza na gazeti hili wiki hii, Profesa Kihampa alisema TCU ilikuwa inakamilisha mapitio ya maombi ya udahili kwa wale waliochaguliwa kwenye chuo zaidi ya kimoja kuona kama wamethibitisha udahili wao kwenye chuo kimoja kutoa nafasi kwa vyuo kufahamu nafasi zilizo wazi za masomo katika fani mbalimbali.Alisema baadhi ya wanafunzi waliomba fani ambazo haziendani na masomo waliyosoma hivyo kukosa nafasi na kuwataka ikiwa fursa hiyo itatokea wanaweza kuomba tena kwa kuzingatia masomo waliyosoma na fani husika.Profesa Kihampa alisema tatizo jingine ni wanafunzi kuomba fani zenye ushindani huku wakifahamu kwamba ufaulu wao katika fani hizo haumudu ushindani.Alisisitiza kwamba lazima mwenye ufaulu wa daraja la kwanza apewe kipaumbele zaidi ya wa daraja la pili au tatu.Alisema ni vyema waombaji wanapoomba fani za kusoma wakaangalia ushindani wa chuo, wingi wa nafasi na pia ufaulu wao kuepuka kukosa nafasi.Oktoba 3, mwaka huu, TCU ilitoa orodha ya majina ya wanafunzi ambao wamedahiliwa kwenye chuo zaidi ya kimoja ambao idadi yao ilikuwa 25,506 na kati ya hao, hadi Oktoba 8, mwaka huu wanafunzi wapatao 8,000 walikuwa hawajathibitisha udahili wao. | 3 |
ELIYA MBONEA-ARUSHA Mvua iliyonyesha kwa takribani saa 10, imezua taharuki katika Jiji la Arusha huku mawasiliano kati yake na Moshi yakikatika kwa saa kadhaa. Jana
katika Jiji la Arusha makazi mengi yalikuwa yamezungukwa na maji huku barabara
zikiwa zimejaa maji hali iliyokwamisha wanafunzi na watu wengine kwenda kwenye
shughuli zao. Pia
wakati wasafiri waliokuwa wakitoka Arusha kuelekea Moshi na Dar es Salaam
walikwama tangu alfajiri jana hadi majira ya saa nne maji yalipopungua
barabarani na magari kuanza kupita. Kukwama
kwa wasafiri hao kulisababishwa na Mto Biriri kufurika maji. Kwa
upande wa mafuruko kwenye Jiji la Arusha, mbali na kufurika katika maeneo ya
watu, kwenye baadhi ya maeneo watu waliripotiwa kusombwa na maji. Mmoja wa waliosombwa ni kijana mmoja aliyechukuliwa na maji kwenye mtaro eneo la Kijenge ambaye alisaidiwa na askari waliokuwa wakiongoza magari katika eneo hilo. Katika
mazingira yasiyotegemewa, kijana huyo aliyekuwa akijaribu kuvuka mtaro mkubwa,
alijikuta akiteleza na kuanza kusombwa na maji kwa umbali wa hatua 20 kabla ya
kuokolewa. Hata
hivyo, mara baada ya kusaidiwa kutoka kwenye maji, kijana huyo aligoma
kujitambulisha majina yake na akasujudu akimshukuru Mungu kwa kumwokoa na kifo.
Kutokana
na mvua hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan Shana, aliwataka
wananchi kuchukua tahadhari zaidi hasa wanapokuta maji mengi barabarani. Alisema
katika maeneo waliyotembelea kujionea hali halisi, hakuna madhara ya kifo
yaliyojitokeza zaidi ya uharibifu wa vifaa vya ndani kama makochi, vyombo,
magari kuangukiwa na kuta za nyumba na miti kuanguka. “Saa
7 usiku, Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo alinipigia simu kunipa maelekezo ya kuingia
barabarani kuhakikisha tunashirikiana na Zimamoto kuokoa watu na mali zao. “Nashukuru
wananchi wametupa ushirikiano mkubwa, na askari wa Zimamoto kwa uhakika
wamefanya kazi kubwa ya kuvuta maji yaliyojaa maeneo yaliyozingira makazi ya
watu,” alisema RPC Shana. Kwa
upande wake, Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Arusha, Kennedy Komba, alisema chanzo
kikubwa cha maji hayo kusimama na kuingia kwenye makazi ya watu ni njia za maji
nyingi kufungwa. “Niwaombe
watendaji wa mitaa na kata tusimamie na kutimiza wajibu wetu, wakati watu
wanapojenga tuhakikishe njia za maji hazifungwi ili kupunguza maafa wakati wa
mvua kubwa. “Niwaombe
wananchi katika kipindi hiki kukitokea maafa yoyote yanayohitaji uokozi, naomba
tuwasiliane kwa namba 114 kwani tukipata taarifa hizi kwa wakati zinaweza
kusaidia kuokoa maisha ya watu na mali zao,” alisema. Naye
Mkazi wa Mtaa wa Osunyai Ngusero, Emmy Proper ambaye nyumba yake ilizingirwa na
maji na kusababisha uharibifu mkubwa wa masofa, vyombo vya umeme na magodoro,
alisema maji yalianza kujaa ndani usiku. “Tumeingiliwa
na maji usiku, hatukulala hapa imebidi tuhamishe watoto mtaa mwingine kuanzia saa
9 usiku, hali ilikuwa mbaya sana, maji yalijaa mpaka usawa wa madirisha,”
alisema Emmy. Mkazi
mwingine wa eneo la Kijenge Kati, Kirenga Swai aliyeharibikiwa magari yake
mawili na nyumba kujaa maji, alisema saa 12:30 asubuhi alistukia kuona gogo
kubwa likisukumwa na hadi kwenye ukuta kisha ukavunjwa na maji kujaa ndani. “Magari
yangu mawili yameharibika kama unavyoona vioo vimepasuka, taa za magari
zimevunjika, maji yamejaa ndani, kila kilichomo humo kimejaa matope hakifai
tena, vifaa vya umeme vimeharibika,” alisema Swai. Aidha
wakati hali ikiwa hivyo, katika baadhi ya mitaa ya Jiji la Arusha na maeneo
jirani hali ilikuwa mbaya zaidi kutokana na magari kushindwa kupita barabarani
kutokana na maji kujaa. Barabara
ya Moshi-Arusha hali haikuwa nyepesi kutokana na maji yakiwa na matope mazito
kujaa eneo la King’ori na maeneo mengine na kusababisha magari mengi kupita kwa
tahadhari. Licha
ya magari kushindwa kupita barabarani kutokana na maji mengi, kwa baadhi ya
wakazi wa Jiji la Arusha hali haikuwa rahisi kwani wengi wao walishindwa kufika
makazini kwa wakati kutokana na maeneo yao kujaa maji. Baadhi
ya wanafunzi wa shule mbalimbali za mjini Arusha nao walijikuta wakipata wakati
mgumu wa kufika mashuleni kutokana na magari yao kukumbwa na kadhia hiyo. Baadhi
yao walishindwa kutoka majumbani mwao kutokana na nyumba kujaa maji, madaftari
kulowana na hivyo kushindwa kwenda shuleni. | 3 |
MTANGAZAJI maarufu na mchambuzi wa michezo ndani na nje ya Tanzania, Ephraim Kibonde aliyefariki dunia jana atazikwa kesho katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.Wadau mbalimbali wa michezo wamejitokeza na kumlilia Kibonde ambaye mbali na kuwa mwanzilishi wa kipindi cha michezo cha Clouds FM, pia ni mchambuzi wa soka wa Super Sports. Mtangazaji huyo mara nyingi mwishoni mwa wiki alikuwa akisafiri kwenda Afrika Kusini kufanya uchambuzi wa mechi za Ligi Kuu ya England katika Studio za Super Sports kwa lugha ya Kiswahili yeye pamoja na watangazaji wengine wa Tanzania.Kifo cha Kibonde kimekuja siku chache baada ya kuwa MC katika msiba na hatimaye maziko ya Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba huko Mikocheni na mkoani Kagera Jumatatu. Mkurugenzi Mtendaji wa CMG, Joseph Kusaga, alisema mwili wa Kibonde ukishawasili Dar es Salaam kutokea Mwanza utapumzishwa kwenye Hospitali ya Jeshi ya Lugalo na Jumamosi utapumzishwa katika makaburi ya Kinondoni.Kwa mujibu wa taarifa ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk Thomas Rutachunzibwa, Kibonde alifariki dunia wakati akipelekwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando kutokea hospitali ya Uhuru, zote za mkoani humo. Kifo cha Kibonde kimekuja ikiwa ni takribani miezi minane baada ya kifo cha mkewe Sarah, aliyefariki kwa ugonjwa wa saratani na kuzikwa makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. | 4 |
MANCHESTER, ENGLAND MSHAMBULIAJI wa timu ya Manchester United, Anthony Martial,
ameweka wazi kuwa, vita yao ya kupachika mabao na Marcus Rashford kutaifanya timu
hiyo ifanye vizuri msimu huu. Safu ya ushambuliaji kwa sasa itakuwa chini ya wachezaji
hao wawili baada ya kuondoka kwa Romelu Lukaku aliyejiunga na kikosi cha Inter
Milan wakati huu wa kiangazi. Wachezaji hao wawili katika michezo miwili waliocheza tangu
kufunguliwa kwa msimu mpya wa ligi wamefanikiwa kila mmoja kufunga mabao
mawili, hivyo Martial anaamini kila mmoja kati yao wana kiu kubwa ya kufunga
mabao. Katika mchezo wao wa kwanza wa ufunguzi wa Ligi Kuu dhidi
ya Chelsea, Rashford alifunga mabao mawili, huku Martial akifunga bao moja
katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Chelsea, wakati huo mchezo wao wa pili dhidi
ya Wolves uliomalizika kwa sare ya 1-1 Martial akifunga bao hilo. “Kwenye mazoezi tumekuwa na ushindani mkubwa wa kufunga
mabao, kila mmoja anataka kuwa kinara wa mabao, hakuna ambaye anapenda kuona
mwenzake akiomuongoza kwenye kufunga bao, kuna wakati Rashford anakuwa kinara na
kuna wakati ninaongoza mimi. “Ushindani huo utakuwa vizuri tukiuendeleza kuufanya katika
michezo ya ligi, hakuna ambaye atakuwa anaumia kuona mwenzake amefunga bao kwa
kuwa kila mmoja ana lengo la kuisaidia timu kufanya vizuri, ninaamini kwa
kufanya hivyo msimu huu tutakuwa na mabao mengi na kuisaidia timu,” alisema
mchezaji huyo. Manchester United leo watakuwa kwenye uwanja wa nyumbani na
kuwakaribisha wapinzani wao Crystal Palace ambapo utakuwa ni mchezo wa tatu
tangu kufunguliwa kwa msimu mpya wa ligi. Martial anaamini wana nafasi kubwa ya
kufanya vizuri kwenye uwanja huo wa nyumbani baada ya kutoka sare ugenini dhidi
ya Wolves. | 4 |
KHARTOUM, SUDAN MAWAZIRI 10 wameambukizwa virusi vya corona nchini Sudan Kusini, msemaji wa serikali amethibitisha kupitia mahojiano yake na Shirika la Utangazaji la Uingereza la BBC. Waziri wa Habari, Michael Makuei amesema wenzake hao tayari wamejiweka karantini Waziri huyo Makuei alisema kuwa mawaziri wote hao walikuwa ni wajumbe wa Kamati ya juu ya Serikali ya kupambana na corona nchini humo. Katika mawaziri waliopo kwenye kamati hiyo, ni Waziri wa Afya pekee ambaye hajakutwa na maambukizi. Inaripotiwa kuwa mawaziri hao wamepata maambukizo baada ya kukutana na aliyekuwa mjumbe wa kamati hiyo ambaye alikuwa na virusi vya corona. Mawaziri wote 10 wamejitenga kwa sasa na serikali imesema kuwa wote wanaendelea vizuri kiafya. Taarifa za kuambukizwa kwa mawaziri hao zinakuja siku chache baada ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi hiyo, Riek Machar kutangaza kuwa amekutwa na virusi hivyo pamoja na mkewe, ambaye ni Waziri wa Ulinzi. Walinzi wa viongozi kadhaa nchini humo wamekutwa na virusi na kwa sasa wapo karantini. ]Hadi sasa zaidi ya watu 300 wamethibitishwa kupata virusi vya corona Sudani Kusini, huku watu wanne wakipona na sita kufariki. Umoja wa Mataifa umetahadharisha juu ya hatari ya kuporomoka kabisa kwa mfumo wa afya wa nchi hiyo ambao una uwezo mdogo kutokana na mgororo wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambao umeathiri ustawi wa maendeleo. Kwa sasa Rais, Salva Kiir wameweka tofauti zao za kisiasa pembeni na kutengeneza serikali ya umoja wa kitaifa, japo hawajaweza kukubaliana katika baadhi ya mambo ya msingi kama udhibiti wa majimbo. Wakati corona ikiendelea kuleta wasiwasi, nchi hiyo pia inakabiliwa na uhaba wa chakula kwa sasa. | 2 |
Na Mwandishi Wetu, SHIRIKA lisilo la kiserikali la Foundation for Civil Society, limeadhimisha siku ya ‘Jumanne ya Kutoa’ maarufu ‘Giving Tuesday’ kwa kutoa misaada mbalimbali katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Dar es Salaam. Shughuli hiyo inaadhimishwa kila Jumanne ya mwisho ya mwezi Novemba duniani kote na kwa hapa Tanzania ni mara ya kwanza kuadhimishwa. Akizungumza katika shughuli hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa FCS, Francis Kiwanga, alisema shirika kwa kutambua umuhimu wa mashirika, makampuni na watu binafsi katika jamii, limeamua kuleta utamaduni huo nchini na hiyo inapaswa kuwa ni moja ya shughuli zinazotakiwa kufanywa na kila shirika walau mara moja katika mwaka. Mkurugenzi huyo alisema wafanyakazi wa shirika hilo waliamua kuchangia shughuli hiyo kwa asilimia moja ya mishahara yao kwa miezi sita na kampeni nzima imesaidia kukarabati choo kimoja kinachotumiwa na wanafunzi wa shule hiyo. Akizungumza katika shughuli hiyo, mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Utawala kutoka katika Wizara ya Elimu, Pancras Steven, alishukuru kwa mchango huo wa FCS. Steven alisema shirika hilo limeonyesha liko makini na kwamba linajali maendeleo ya kila watu na hasa walio na uhitaji zaidi. “Kazi hii mliyofanya ni kubwa, nawapongeza, nitumie nafasi hii kuwaomba Watanzania kujenga utamaduni wa kuchangia katika majukumu ya maendeleo katika jamii. “Kwa kufanya hivi mnasaidia sana kuhamasisha jamii nasi kama Serikali tunaungana nanyi,” alisema. Mwalimu Mkuu wa Uhuru Mchanganyiko, Anna Mshana, aliishukuru FCS kwa kuichagua shule hiyo. Alisema shule hiyo ina uhitaji mkubwa ikizngatiwa wanafunzi wanaosoma katika shule yake ni tofauti na wanaosoma katika shule nyingine. | 3 |
WASTANI wa watoto 394 hubakwa kila mwezi katika maeneo mbalimbali Tanzania Bara.Pia imeelezwa kuwa ulawiti wa watoto umeongezeka kwa matukio 545 kwa mwaka 2017/18, ambapo mikoa inayoongoza kwa matukio hayo ni Dar es Salaam na Iringa.Takwimu hizo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).Ripoti hiyo inaonesha matukio ya ukatili wa kingono miongoni mwa watoto yanaongezeka nchini.Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi alisema hayo katika taarifa yake inayoelezea uzinduzi wa Kampeni ya Ulinzi wa Mtoto dhidi ya Ukatili wa Kingono, utakaofanyika kesho jijini Dar es Salaam.Liundi alisema vitendo hivyo havikubaliki katika jamii, kwani ni kinyume cha haki za binadamu na mikataba mbalimbali ya kimataifa na kikanda iliyoridhiwa na serikali juu ya ulinzi wa mtoto dhidi ya aina zote za ukatili wa kijinsia.“Vitendo hivi vinarudisha nyuma maendeleo ya mtoto na taifa kwa ujumla. Miongoni mwa athari zitokanazo na ukatili wa kingono dhidi ya watoto ni pamoja na watoto kuathirika kisaikolojia, maambukizi ya magonjwa ya zinaa na ukimwi, mimba za utotoni na kubwa zaidi ni kuhatarisha ustawi wa taifa na kuchochea uongezeko la vitendo katika jamii,” alisema.Amesema kutokana na takwimu hizo tatizo ni kubwa na limesukuma mtandao huo kuzindua kampeni hiyo, ambayo itachangia katika jitihada za serikali kutokomeza aina zote za ukatili dhidi ya watoto.Amesema lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu kwa jamii juu ya athari za ukatili wa kingono kwa watoto na umuhimu wa kuwalinda dhidi ya aina hiyo ya ukatili, kutathmini na kuibua mijadala katika jamii juu ya hali halisi ya ukatili wa kingono.Pia kuhamasisha jamii kuzuia vitendo hivyo visitokee na kutoa taarifa mara waonapo matukio hayo ya ukatili wa kingono kwa watoto ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua stahiki. | 3 |
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vya siasa nchini kutopeleka malalamiko yao katika vyombo vya habari kuhusu masuala ya uchaguzi na badala yake viwasilishe hoja hizo katika Kamati za Maadili za Uchaguzi.Imesema haina mfumo wa kushughulikia malalamiko ya uchaguzi kupitia vyombo vya habari badala yake imetaka utaratibu wa kisheria kufuatwa ili haki itendeke kwa wote. Mkurugenzi wa NEC, Dk Athuman Kihamia alisema hayo akiwasilisha mada ya Uboreshaji daftari la kudumu la wapigakura katika semina ya viongozi wa vyama vya siasa, dini, walemavu, vijana, wanawake, asasi za kiraia na watendaji wa NEC.‘’Pamoja na uwepo wa Kamati za maadili zenye mamlaka ya kutatua migogoro na kuweka mazingira sawa ya ushindani katika chaguzi ndogo, vyama vimekuwa havipeleki malalamiko yao kwenye kamati hizo bali hutoa malalamiko yao kupitia vyombo vya habari, ‘’ alisema. Alizitaja kamati zinazoundwa wakati wa uchaguzi kuwa za maadili ya uchaguzi, kamati ya rufaa, kamati ya maadili ya kitaifa, kamati ya maadili ya jimbo na kamati ya maadili ya kata.Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage alisema kifungu cha 15 (5) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, sura ya 343 kikisomwa na kifungu cha 21 (5) cha Sheria ya uchaguzi ya serikali za mitaa kinaipa NEC mamlaka kuboresha daftari la kudumu la wapigakura. Alisema pia NEC iliendesha uhakiki wa vituo vya kuandikisha wapigakura nchini ambapo kwa mkoa wa Kilimanjaro, iliongeza vituo vya kujiandikisha kutoka vituo 1,273 hadi 1,286.Mwenyekiti wa wanahabari Kilimanjaro, (Mecki), Bahat Nyakiraria aliomba tume kuhakikisha makundi maalumu yanapewa kipaumbele kama ilivyokusudiwa. Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), mkoa wa Kilimanjaro, Awadhi Lema alitaka NEC kutoa matangazo ili wale waliopoteza kadi za kura wapate kadi mpya. | 3 |
Na MWANDISHI WETU – dar es salaam
TANGU Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda atangaze orodha mpya ya watu 65 iliyojumuisha wanasiasa na watu wengine maarufu Jumatano wiki hii, na kuwataka wafike Kituo Kikuu cha Polisi wakajadiliane juu ya tuhuma za dawa za kulevya, kiongozi huyo hajaonekana tena hadharani.
Tofauti na wiki iliyopita wakati alipotangaza kwa mara ya kwanza orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya iliyowajumuisha askari polisi 17, wasanii na watu mbalimbali 18, Makonda alikuwa akionekana polisi kwa uwazi na hata kuelezwa kushiriki mahojiano na watuhumiwa hao.
MTANZANIA Jumapili limebaini kuwa tangu atangaze awamu ya pili ya watuhumiwa hao 65, Makonda hajaonekana na wala hajakutana na watuhumiwa hao.
Si hilo tu, pia hajafanya mikutano na waandishi wa habari kueleza nani kafika na nani hajafika miongoni mwa watuhumiwa hao.
Taarifa hizi zinathibitishwa pia na Askofu wa Kanisa na Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, ambaye muda mfupi baada ya kuachiwa jana jioni, aliliambia MTANZANIA Jumapili kuwa hajawahi kukutana wala kuonana na Makonda katika mahojiano kituoni hapo tangu aliporipoti Alhamisi wiki hii.
Mara baada ya kutangaza orodha ya kwanza, Makonda alifika mara kadhaa kituoni hapo na hata kufanya mkutano na waandishi wa habari akiwa ameambatana na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro.
Katika mkutano huo ambao Makonda aliutumia kueleza matarajio yao ya kuwafikia wauzaji wakubwa wa dawa za kulevya, pia aliwataja watuhumiwa walioripoti na ambao hawakuripoti.
Zaidi aliutumia mkutano huo kuwaongeza kwenye orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya, mwanamuziki Vanessa Mdee, mrembo anayependezesha video za muziki, Tunda na askari wengine watano ambao nao aliwataka wafike kuripoti kituoni hapo Jumatatu ya wiki iliyopita.
Ingawa zipo taarifa ambazo hazijathibitishwa kwamba Makonda alifika kituoni hapo juzi, lakini alifanya hivyo kimya kimya.
Juzi ikiwa siku moja baada ya watuhumiwa wawili kuripoti kituoni hapo na kuwekwa ndani, Kamanda Sirro alifanya mkutano na waandishi wa habari chini ya mti uliopo nje ya kituo hicho cha polisi pasipo uwepo wa Makonda.
Sirro aliitaja orodha ya watu waliofika hadi kufikia juzi kuwa ni wanne tu kati ya 65 waliokuwa wametajwa na Makonda.
Jana ikiwa ni siku tatu tangu Makonda atangaze orodha hiyo ya awamu ya pili, lakini pia Jeshi la Polisi likimwachia Askofu Gwajima, bado kiongozi huyo alibaki kimya zaidi ya kutuma picha kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, ikimwonyesha akiwa nyumbani kwake na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Khalid Mohamed ‘TID’.
TID ni miongoni mwa wasanii na watu mbalimbali 18 ambao Makonda aliwatangaza kwenye sakata la dawa za kulevya katika orodha ya kwanza wiki iliyopita.
Msanii huyo ni miongoni mwa wale ambao walifikishwa mahakamani mwanzoni mwa wiki hii kutokana na kosa la kujihusisha na dawa za kulevya.
“Mungu wetu hajalala na siku zote anampenda amtafutae, karibu tena nyumbani TID.” aliandika Makonda katika mtandao wake wa Instagram.
Picha kama hiyo pia aliiweka TID katika ukurasa wake wa Instagram ikiwa imebeba maandishi yanayosomeka: “Muziki bila madawa ya kulevya inawezekana… This is the turning Point kwangu mimi na kizazi cha mziki huu wa kizazi kipya, nikiwa na Mh. Makonda leo tukijadili Jinsi gani ya kuokoa vipaji na sanaa kwa ujumla, Mungu ibariki Bongo Fleva, Mungu Ibariki Tanzania”.
Mara kadhaa MTANZANIA Jumapili lilimtafuta Makonda ofisini kwake na kupitia simu ya mkononi bila mafanikio.
Tangu aibuke wiki iliyopita na operesheni ya kupambana na dawa za kulevya katika mkoa wake wa Dar es Salaam, Makonda ametaja orodha mbili tofauti za watuhumiwa wa dawa hizo.
Wakati akitangaza orodha ya pili, Makonda alisisitiza kuwa habahatishi na kwamba watu aliowataja tayari wamefanya uchunguzi wa kutosha dhidi yao.
Kampeni hiyo ilionekana kugusa moja kwa moja mamlaka za juu baada ya hivi karibuni Rais Dk. John Magufuli wakati akimwapisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, kutumia fursa hiyo kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuingia katika vita hiyo na kuhakikisha kila anayehusika anakamatwa bila kujali umaarufu wake.
Kabla ya kauli hiyo ya Rais Magufuli, operesheni hiyo aliyoianzisha Makonda ilionekana pia kuigusa Wizara ya Mambo ya Ndani.
Katika hatua ambayo pengine haikutarajiwa na wengi, ikiwa ni siku tatu tu tangu Makonda aanze operesheni yake, Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu alitangaza kuwasimimamisha kazi askari 12 ambao majina yao yalitajwa kwenye orodha ya Makonda Alhamisi na Ijumaa ya wiki iliyopita.
Hata hivyo, upepo ulionekana kuvuma vibaya upande wa Makonda baada ya suala hilo kufika bungeni ambako baadhi ya wabunge walimpinga vikali kwa hoja kwamba operesheni yake hiyo ilikuwa haijazingatia misingi ya kisheria.
Wakati Bunge likiwa na mtazamo huo, baadhi ya watu wanaomuunga mkono walikuwa na hoja kwamba Makonda ndiye mtu pekee aliyethubutu kuwataja kwa majina watuhumiwa tofauti na viongozi wengine waliopita. | 3 |
Bethsheba Wambura, Dar es Salaam Uzinduzi wa Filamu ya Salamu iliyowashirikisha waigizaji Irene Uwoya, Stephen Almasi, Cojack Chilo maarufu Shaka Zulu na wengine wengi unatarajiwa kufanyika Jumamosi Machi 3, mwaka huu jijini Dar es Salaam. Filamu hiyo inayoelezea stori ya watoto wadogo wanaotumika kama chambo katika kufanya uhalifu wa mazao na mifugo. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 25, mwandishi na muongozaji wa filamu hiyo Salum Majagi amesema watoto waliocheza humo wanawawakilisha watoto wengine wanaofanyishwa kazi na watu wazima ili kujipatia kipato. “Tanzania ni moja ya nchi ambazo watoto wanatumikishwa sana hivyo sisi kama wasanii tumeona tutumie sanaa kuikumbusha jamii kuhusu tabia hizi na ndiyo maana tumekuja na filamu ya Salamu,” amesema. Majagi ambaye pia ndiyo muongozaji wa filamu ya Siyabonga iliyoshinda kama Filamu Bora na Filamu yenye maudhui ya kitaifa katika Tuzo za Kimataifa za Sinema Zetu (SZIFF) zilizofanya jijini Dar es Salaam Juzi Jumamosi Februari 23, amesema katika uzinduzi huo yatakuwepo makampuni mbalimbali ya kimataifa hivyo amewasihi washabiki wa filamu kufika kwa wingi. Aidha amesema tiketi zitapatikana kwa bei ya Sh 10,000 kawaida na 20,000 VIP na uzinduzi utafanyika City Mall jijini hapa. Naye mmoja wa waigizaji wa filamu hiyo Cojack Chilo, amesema katika filamu hiyo wamezingatia kila kitu ili kuongeza ubora kuanzia stori, ubora wa picha na mazingira hivyo amewasihi Watanzania kufika siku hiyo na kushuhudia uzinduzi huo. | 1 |
SWAGGAZ RIPOTA, MARA chache mno msanii mkubwa kuweka imani kwa msanii mchanga na kuamua kumpa mamlaka kamili kwenye ngoma yake anayoitegemea. Licha ya unadra huo, Bongo tumebahatika kuwa na msanii wa namna hiyo ambapo alifanikiwa kuwa staa muda mfupi tu mara baada ya kushirikishwa kwenye Uswazi Take Away, ngoma ya msanii Chege. Huyu ndiyo Malaika Exavery au Malaika. Kama ilivyo kawaida ya jarida hili kukuletea mastaa mbalimbali wa Bongo leo tupo na mrembo huyu, mkali wa ngoma kama Mwamtumu, Sare Sare, Zogo na Ralua inayofanya poa hivi sasa. MALAIKA NI NANI Anasema yeye alizaliwa huko Bukoba kwenye kijiji kinachoitwa Ibwela na baadae akahamia Arusha na kukulia huko. Alisoma shule ya msingi hapa Dar es salaam lakini elimu ya Sekondari alikwenda kuimalizia tena Arusha. “Wakati nipo shule tayari mambo ya urembo yalinitawala hivyo nikashindwa kufanya vizuri mtihani wangu wa mwisho kitu ambacho familia yangu pia ilikishangaa mno. Nilirudi Dar kuanza kutafuta mkwanja na kwenye harakati zangu nikakutana na Adam Juma ndiyo nikapata dili la kuwa ‘Make up Artist’ wake, ”. Nilisoma kozi fupi na nikawa keshia pale RITA, ambako sikukaa sana nikaajiriwa kwenyetaasisi zingine kisha nikasafiri kwenda China na baadae India, wakati huo Uswazi Take Away niliyofanya na Chege ilikuwa inafanya poa na ni kama nilikuwa nimepishana na bahati sababu wengi walitaka kunifahamu ila mimi sikuwapo nchini,” anasema. MAAJABU YA MWAMTUMU BAADA ya kurejeanchini akitokea India, Malaika alirekodi ngoma yake ya Mwamtumu. Wimbo huu ulimshangaza kwani licha ya kumuingiza kwenye kinyang’anyiro cha tuzo za KTMA, tena kwenye kipengele kigumu cha Msanii Bora wa Kike, Mwamtumu ilipendwa zaidi Ulaya na Marekani kuliko hapa Bongo. “Nilipotoa Mwamtumu kwa hapa nyumbani haukufanya vizuri ila huko Texas, Marekani na nchi zingine za Ulaya ulifanya vizuri sana kwa hapa Bongo haukufanya vizuri ila nilipotoka Sare sare ndiyo watanzania waliuelewa,” anasema Malaika. SHOO KIBAO ANAFUNIKA ILA HII ALIZINGUA Malaika anasema kabla hajafanya shoo huwa anatetemeka kwa uoga ila akishapanda jukwaani hofu inapotea na anapiga shoo yenye ubora mkubwa na akishuka tena jukwaani huanza tena kutetemeka. Licha ya kufanya shoo kali na classic kuna siku alizingua siku hiyo alitambua kuwa aliharibu. “Kuna shoo niliifanya Zanzibar, nakumbuka nilikuwa nimetoka safari nje ya nchi, ile nimetua tu na ndege nikaenda Arusha harafu nikapitiliza mpaka Zanzibar. Nilichoka sana pia watu ambao huwa wananiandaa kabla ya shoo walikuwa hawajaweka sana baadhi ya vitu hiyo ikafanya nitumbuize chini ya kiwango. SIRI YA KULAMBA MASHAVU SERIKALINI, BALOZI UNAWEZA ukashangaa kwanini idadi ya wasanii wanaoonekana kwenye hafla za serikali na zile za balozi za nchi mbalimbali ni ndogo. Heshima pamoja na nidhamu ni kigezo moja wapo kinachompa msanii shoo za kiserikali na zile zinazoandaliwa na balozi ambazo mkwanja wake ni mrefu tofauti na zile za kwenye klabu. “Kama msanii umezoea kuvaa vichupi huwezi kupata dili za matangazo kwenye Serikali, balozi na taasisi za heshima ila huko kwenye kampuni zinazotengeneza nguo za ndani utapata, Siri kubwa ya mimi kutumbuiza kwenye shunguli za kiserikali na kwenye balozi za nchi kama Uingereza, Ujerumani, Burundi, Norway na nyingine ni profile yangu nzuri kwa jamii,” anasema Malaika”. UGENI WA JPM NYUMBANI KWAKE February 18 mwaka huu, Malaika anasema hawezi kuisahau siku hiyo kwa kuwa alitambua kuwa muziki wake una thamani kubwa duniani mara baada ya Rais John Pombe Magufuli (JPM), kumtaja kama msanii anayemkubali alipowaalika wasanii pale Ikulu ya Magogoni. “Nilifurahi mno kutajwa na Rais ila nilisikitika kwa kuwa sikuhudhuria. Nilikuwa kwenye Tv naangalia. Siyo hivyo tu aliwatuma watu wake waje nyumbani kwetu kuchukua CD za nyimbo zangu. Imagine unaona magari ya Ikulu yamekuja kwenu kutaka kazi yako ambayo Rais ameagiza ipelekwe kwake. Kwangu mimi ni kitu kikubwa hata leo akitokea mtu akisema sijui kuimba nitamdharau mno,” alisema Malaika. TUKIO LILILO MUUZIZA MOJA ya kitu ambacho hawezi kukisahau na kilimuumiza ni pale alipoambiwa yeye siyo mtanzania na maafisa wa usalama kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Nyerere. “Majina yangu naona yaliwazuzua na wakadhani mimi siyo mtanzania. Nilizuiliwa kusafiri mpaka nilete udhibitisho wa vyeti vyangu vya kuzaliwa ili wathibitishe kama mimi ni raia wa Bongo. Niliwaletea ila hata waliponiruhusu kuondoka nilikuwa nimechelewa michongo niliyotaka kwenda kuifanya”. ACHOMESHWA MAHINDI AIRPORT CHINA Malaika, anasema kuna siku aliwahi kukaa masaa 16 kwenye uwanja wa ndege nchini China, mara baada ya kuhisiwa amebeba dawa za kulevya. Simu na mizigo yake ilichukuliwa ili ikakaguliwe na kwa muda huo mtu aliyetakiwa kumpokea, alikata tama na kuamua kuondoka kitu ambacho kilimpa msukosuko kwenye nchini hiyo ukizingatia yeye ni mgeni. KAMA WEWE NI MASIKINI HUWEZI KUMNASA Miezi miwili iliyopita alimuacha mpenzi wake na kuamua kuwa singo ili awekeze nguvu kwenye kutafuta mkwanja zaidi. Malaika anasema hajawahi kufikiria kutoka kimapenzi na mtu masikini labla masikini huyo awe na mipango ya kutengeneza fedha. “Kwa sasa sipo tayari kuwa na mpenzi. Ila sifa za mwanaume ambaye anaweza kuwa na mimi ni yule mwenye uelewa wa mambo mengi awe muelewa wa mambo mengi na kingine huwa sidili kabisa na mwanaume masikini labla akitokea awe na mipango ambayo itaweza kutuingizia fedha,” alisema. UTATA SKENDO YA KUWA FREEMASON Amekuwa akihusishwa kuitumikia jamii ya siri ambayo inasemekana humuabudu shetani ‘Freemason’. Swaggaz lilitaka kufahamu kama ni kweli au laa na kama siyo kweli yeye huwa anasali au anaswali “Hivyo vyote mimi sifanyi ila namuamini Mungu. Unajua huwenda kuna watu uliokuwa unakula nao chipsi za jero na ice cream za mia mia sasa wameona maisha yako yamebadilika tena ghafla ndiyo wanaanza kuongea maneno hayo ila itafika muda nitalizungumza kwa kina jambo hili kwa sasa sipo tayari,” anasema. IMEANDIKWA NA JOHANES RESPICHES NA CHRISTOPHER MSEKENA. | 1 |
OMBAOMBA 43 wamekamatwa na katika Mkoa wa Mjini Magharibi na kati yao 13 wanatoka Tanzania Bara na kazi ya kuwarudisha makwao ikianza.Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud alisema hayo wakati akizungumza na ombaomba hao waliokusanywa pamoja ili kubaini undani wao na kuwarejesha makwao.Alisema kazi ya kuwatafuta na kuwabaini ilianza baada ya ombaomba hao kuenea kwa kasi katika viunga vya Mkoa wa Mjini Magharibi. Baadhi yao walionekana kukaidi maagizo mbalimbali yaliyotolewa hapo awali na uongozi wa mkoa huo ya kuacha shughuli hiyo. Mahmoud alisema kazi ya kuwakusanya ombaomba katika mkoa wake, imefanikiwa na kusisitiza shughuli hiyo haikubaliki katika maeneo hayo. Alisema mtu yeyote atakayekamatwa akifanya shughuli hiyo, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.Alisema Serikali ya Zanzibar inaendelea kuwajengea mazingira bora wananchi wake ikiwemo kuimarisha ustawi wa jamii, hivyo si vyema baadhi ya wananchi kufanya mambo yasiyokubalika. Mkuu wa Mkoa alisema uchunguzi uliofanywa, umebainisha kuwepo kwa baadhi ya watu wanaoleta watu kufanya biashara hiyo kutoka maeneo mbali mbali kwa lengo la kujipatia kipato.Kwamba jambo hilo ni kinyume na utaratibu wa sheria za nchi. Pia alisema tabia hiyo inaharibu mila na utamaduni wa Kizanzibari. Mapema akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Ustawi wa Jamii na Idara ya Wazee, Wahida Maabadi alisema tabia ya kuombaomba inatia aibu serikali, kwani imekuwa ikijitahidi kuandaa mazingira mzuri ya kusaidia watu wasiojiweza na wenye mahitaji maalum.Baadhi ya ombaomba hao, wengi wao wakiwa wanawake, walieleza kuwa hali duni, kukosa msaada na ugumu wa maisha, ndivyo vinachangia wao kufanya kazi hiyo. Waliomba radhi uongozi wa serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi na kuahidi kutoendelea na jambo hilo. | 3 |
MWIGIZAJI wa filamu nchini Wema Sepetu ameiomba radhi Serikali, Bodi ya filamu, familia, mashabiki wake na watanzania kwa ujumla kutokana na makosa yake ya kusambaza video zake chafu kwenye mitandao ya kijamii.Tangu wiki iliyopita kumekuwa na video chafu za faragha zinamuonyesha Wema akiwa na mwanaume zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii katika kurasa za watu mbalimbali ikiwemo ya kwake mwenyewe Wema.Akizungumza na waandishi wa habari jana Wema ambaye alionekana mwenye huzuni kubwa, alisema anakiri kuwa amekosa kwa kuwadhalilisha na kuwafedhesha wengi akisema kilichotokea kimemuumiza na kumpa somo kubwa.“Sihitaji kumlaumu yeyote, kosa ni kosa haijalishi ilikuwaje, siombi radhi kwa kutafuta huruma ya mtu yeyote bali kukiri kuwa nililofanya ni baya. Huenda ni vitendo vya kawaida au vinavyofanywa na wote lakini vinapotoka nje huwa vinaleta taswira tofauti na isiyopendaza,” amesema.Alisema kitendo hicho ni zaidi ya aibu na kinapaswa kilaaniwe vikali na kukiri kuwa huenda anaweza asieleweke kutokana na historia ya maisha yake yaliyopita.Wema alisema anashukuru yaliyotokea sasa kwani tangu ameingia kwenye dunia ya umaarufu mwaka 2006 alipotwaa taji la Miss Tanzania, amegundua kuwa amefanya utoto na ujinga mwingi ambao umekuwa ukiwavunja nguvu watu waliokuwa nyuma yake hata wale wasiomuunga mkono.“Kwasababu labda sikuona athari ya vitu, na mimi naathirika vipi, lakini mara nyingi tunahitaji kufinywa ili uamke, nakiri nimefinywa hasa,” alisema na kuongeza kuwa tangu juzi amekuwa hayupo sawa akitafakari mwelekeo wa maisha yake akiahidi kutorudia makosa ya aina hiyo. | 4 |
WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa, Simba na Mtibwa Sugar leo wako kwenye miji tofauti kupeperusha bendera ya taifa..Simba inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, itakuwa ugenini Kitwe, Zambia kumenyana na Nkana Red Devils ya huko katika mechi ya kwanza huku Mtibwa inayoshiriki michuano ya Kombe la Shirikisho ikiwa Kampala, Uganda kumenyana na KCCA ya Uganda.Simba na Nkana zinakutana kwenye hatua hiyo kufuaitia kufanya vizuri kwenye mechi zao za raundi ya awali Simba ikipata ushindi wa jumla wa mabao 8-1 dhidi ya Mbabane Swallows ya eSwatini wakati Nkana iliitoa UD Songo ya Msumbiji kwa mabao 3-1.Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na ubora wa timu zote mbili hasa kwenye eneo la kiungo na ushambuliaji ambapo kila upande unaonekana kuwa na watu makini na hatari wanaohitaji uangalizi makini. Kwenye eneo la kiungo Simba itamtegemea zaidi Cletous Chama, aliyefunga mabao matatu kati ya manane kwenye mchezo wa hatua ya awali ingawa haitokuwa rahisi sana kwake kutokana na wapinzani wao Nkana kumjua vizuri kwakua amekuwa akiichezea timu hiyo kabla ya kujiunga na Simba.Kocha wa Simba Patrick Aussems, amesema wanaingia kwenye mchezo huo akijivunia maandalizi waliyofanya tangu kumalizika kwa mchezo wao wa mwisho dhidi ya Mbabane Swallows Desemba 5 mwaka huu.Aussems alisema wamejipanga vya kutosha kuhakikisha wanaendeleza pale walipoishia kwenye mchezo uliopita na pamoja na ubora waliokuwa nao wapinzani wao lakini watacheza kwa kushambulia ili kuvuruga mipango ya wenyeji wao. “Najua tumekuja kucheza na timu nzuri na bora yenye uzoefu wa kutosha kwenye michuano hii lakini hilo siyo kikwazo cha kutukwamisha tusifanye kile kilichotuleta huku wachezaji wangu wapo vizuri na nimewajenga katika nyanja zote namaanisha kimbinu na kiakili hivyo nina matarajio makubwa ya ushindi,” alisema Aussems.Kwaupande wake nahodha wa Simba John Bocco, alisema ni mchezo mgumu kwao lakini amejipanga kupambana ili kurudi na ushindi ambao utawaweka katika mazingira mazuri ya kutinga hatua ya makundi ya michuano hiyo ya Caf. Safu ya ulinzi ya Simba ambayo inatarajiwa kulindwa na Aishi Manula, Erasto Nyoni na James Kotei inatakiwa kuwa makini na mshambuliaji hatari Waler Bwalya ambaye ndiyo anaonekana kuwa hatari kwenye ufungaji.Hata hivyo umakini unahitajika katika mechi hiyo kwani Nkana imeshawahi kucheza na Simba mara kadhaa miaka ya nyuma kwenye michuano hiyo na kuisumbua, ikiwemo kuwahi kuifunga mabao 4-0. Kwa upande wa Mtibwa Sugar, kocha wake Zuberi Katwila alisema anafahamu uzuri wa wapinzani wao lakini wamejipanga kupata matokeo ili wasonge mbele.“Najua tuna wapinzani wazuri na mechi itakuwa ngumu kutokana na soka ya Afrika Mashariki kufanana, lakini sijali hilo nimewafundisha wachezaji wangu wanajua nini cha kufanya, nina uhakika wa kupata matokeo,” alisema kocha huyo ambaye aliwahi kuichezea Mtibwa kwa mafanikio makubwa.Mtibwa ambayo iliiondosha Northen Dynamo ya Shelisheli kwenye mchezo wa awali ukiacha uzoefu na wachezaji wa kimaaifa kutoka mataifa ya nje ni timu ambayo imejipanga vizuri na inaundwa na wachezaji wengi vijana waliokaa pamoja kwa muda mrefu hivyo mchezo huo unaarajiwa kuwa mgumu na wenye ushindani mkubwa licha ya kucheza ugenini. Mtibwa inashiriki michuano ya kimataifa kwa mara ya kwanza baada ya zaidi ya miaka 10. | 4 |
Wananchi katika Wilaya tatu za Pemba wasema elimu ya upatikanaji wa huduma za kisheria umewasaidia kupata haki zao za msingi ikiwemo vitambulisho vya mzanzibari mkaazi na vyeti vya kuzaliwa jambo ambalo lilikuwa ni changamoto kwao.Akizungumza Bi Maulidi Saleh wa kijiji cha Kiuyu Minungwini Wilaya ya Chake amesema hapo awali upatikanaji wa huduma hio haukujulikana huku wananchi wakisumbuka kuitafuta huduma hiyo ambayo Mradi wa Uwajibikaji Zanzibar PAZA umekuja kuwafungua macho na kuwa mkombozi baada ya kuwaonyesha njia.Maulid Saleh amesema mradi wa PAZA umewapa elimu ya jinsi ya kupitia njia za kisheria ili kufanikisha upatikanaji wa huduma ambazo zimekuwa ni changamoto ndani ya jamii zao,huku upatikanaji wa vitambulisho na vyeti vya kuzaliwa ilikuwa upatikanaji wake ni wa kusuasua huku wengine wakikosa kabisa ,hali ambayo kwa sasa imeimarika.“Huko nyuma hali ilikuwa ni mbaya sana watu tukiitaabika sana kupata vyeti vya kuzaliwa mtu aweza fika miaka 15 mpaka 18 hajapati chetiche cha kuzaliwa ila mosi izi si haba vyapatikana kwa uharaka baada ya kuonyeshwa mule mwa kupita na namna ya kuziweka wazi changamoto zetu na PAZA”alifafanua bi Maulid Upatikanaji wa huduma hiyo muhimu kwa wazanzibar hivi sasa umekuwa rahisi kwani wamekuwa wakifata njia zile ambazo walionyeshwa na mradi wa PAZA takriban wananchi wengi sasa wanapata vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya Mzanzibar tofauti na pale awali,Aliongeza Bw Shaib Gulam wa shehia ya Kiungoni wilaya ya Wete.Aidha bi Umu lkheri wa Tumbe Wilaya ya Micheweni nae amefahamisha kuwa mbali katika wilaya hiyo kukabiliwa na changamoto kadhaa suala la upatikanaji wa vitambulisho vya mzanzibar mkaazi na vyeti vya kuzaliwa wamepata suluhisho kufatia elimu waliyopewa na mradi ambao wanaouita mkombozi kwani umeleta Mapinduzi ndani ya kijiji chao cha Tumbe na Wilaya kwa ujumla. Mradi wa Uwajibikaji Zanziba ryaani Promoting Accountability in Zanzibar kwa lugha ya kimombo ni mradi ulioshirikisha jumuiya tatu ikiwemo jumuiya ya uhifadhii wa mali asili Pemba NGENAREKO ,jumuiya ya waaandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar WAHAMAZA na chama cha waandishiw aHabari wanawake Tanzania upande wa Zanzibar TAMWA. | 3 |
ANDREW MSECHU -DAR ES SALAAM MBUNGE wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema) amemuomba radhi Katibu Mkuu mstaafu wa CCM , Abdulrahman Kinana kutokana na tuhuma dhidi yake alizowahi kuzitoa bungeni kwa kuwa hazikuwa na ukweli wowote. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam jana, Msigwa alisema anakiri mbele ya Watanzania, kwamba tuhuma hizoalizowahi kuzitoa mara kadhaa dhidi ya Kinana hazikuwa na ukweli wala ushahidi wowote. “Taarifa nilizopewa na kuzitumia hazikuwa na ukweli bail zilikuwa na malengo potofu ya kisiasa na kizandiki. Nasikitika kwamba taarifa hizo nilipewa na watu waliokuwa na malengo maovu. “Mambo kama haya hutokea katika jamii na maishani. Nasi kama binadamu inapotokea kuwakosea wenzetu busara hututuma kuomba radhi na kwa waliokosewa kuwa tayari kusamehe. “Ni dhahiri kwamba kupitia kauli zangu za huko nyuma dhidi yake, nimemkosea, nimemdhalilisha na kumkashifu ndugu yangu Kinana. Nafurahi kuwaambia hapa kwamba nimekutana na kaka yangu Kinana na kumuomba radhi yeye binafsi na amekubali kunisamehe. Baada ya msamaha huo wa Kinana, sasa shauri hili la kimahakama sasa litakuwa limemalizika rasmi,” alisema. Alisema itakumbukwa kwamba kutokana na tuhuma hizo alikuwa na kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania iliyofunguliwa na Kinana dhidi yake kwa sababu ya matamshi aliyowahi kuyatoa dhidi yake ndani na Bunge, akimhusisha na biashara ya ujangili na uuzaji wa nyara za Serikali. Msigwa alieleza kuwa katika hotuba yake akiwa Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni akiwasilisha maoni yao wakati wa mjadala wa makadirio ya matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii ya mwaka 2013/2014, alitoa maelezo marefu ya kumhusisha Kinana na biashara hizo. Alisema kutokana na tuhuma zakeu hizo kwake, Kinana alinifungulia mashitaka katika Mahakama Kuu ya Tanzania kwa shauri namba 108 ya mwaka 2013. “Nimekuja hapa hadharani kuomba radhi kwa sababu nafahamu aliyeumizwa si Kinana peke yake, bali familia yake, ndugu zake, marafiki zake na Watanzania kwa ujumla wao,” alisisitiza. Kabla ya kupeleka suala hilo mahakamani, Kinana kupitia kwa wakili wake, Erick Sikujua Ng’maryo, alimtaka Msigwa kufuta kauli zake hizo na kuomba radhi hadharani kwa kuwa kauli zake hizo hazikuwa na ukweli wowote. Msigwa alikataa kufanya hivyo na kusema yuko tayari kujitetea mahakamani. Jaji Zainab Muruke aliyesikiliza na kuamua kesi hiyo, alieleza kitendo cha wanasiasa kutoa kauli za kudhalilisha wenzao pasipo kuwa na ushahidi wala ukweli wowote kama “tabia mbaya” inayopaswa kukemewa. | 3 |
Na CHRISTOPHER MSEKENA HABARI kubwa kwenye anga la burudani mjini ni shoo ya wakali wa dansi Bongo, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na Johnson Viking ‘Papii Kocha’, itakayofanyika leo kwenye Ukumbi wa King Solomoni, jijini Dar es Salaam. Shoo hiyo ni ya kwanza tangu watoke jela baada ya kukaa kifungoni kwa miaka 14. Weka hiyo pembeni, unawakumbuka Yamoto Band? Ni zilipendwa, kwa sasa kundi hilo limevunjika na kila msanii anafanya kazi zake binafsi. New brand town kwa sasa ni The Mafik, kundi lililopewa heshima ya kipekee leo kutumbuiza kwenye onyesho hilo la wakali, baba na mwana. THE MAFIK NI NINI? Kundi hili ambalo limefanikiwa kujizolea mashabiki wengi kupitia singo yake ya kwanza Passenger, linamikiliwa na uongozi mkubwa huku miongoni mwa washika dau wake wakiwa ni staa wa Bongo Fleva, Nurdin Bilal ‘Shetta’, Kapasta na Mx Carter meneja biashara aliyesimama nyuma ya mafanikio ya wasanii wengi akiwamo Aslay. “Neno The Mafik lina maana ya bahati kwa hiyo wanaounda kundi hili wana bahati maana baada ya kufanya usahili ndiyo tukawapata hawa Rhino King, Hamadai na Mbalamwezi wanaounda kundi hilo na hii siyo bendi japo lina uwezo mkubwa wa kutumbuiza na vyombo vya muziki,” anasema Shetta alipozungumza na Swaggaz. VIPI KUHUSU PESA, WANAWAKE? Baada ya uzinduzi mkubwa wa The Mafik uliofanyika Februari 3, mwaka huu Club Next Door Masaki Dar es Salaam na mastaa mbalimbali kuhudhuria, picha iliyojengeka ni ile inayoonyesha hawana mipaka na hawafungamani na upande wowote. “Kwanza kabisa wana mwaka mmoja na nusu tangu wajuane, tumewanjenga, tumewapa mbinu ambazo zinavunja makundi mengi kwa sababu mara nyingi huwa ni pesa au wanawake. Tunaamini sisi tupo katika umoja na lengo ni kuwafikisha mjini The Mafik,” anasema Shetta. MGAWANYO WA KAZI Rhino King anasema kinacholitofautisha Kundi la The Mafik na wengine ni kwamba wasanii wake kuwa na uwezo mkubwa wa kuimba, kutunga na kucheza vyombo vya muziki, kitu ambacho ni adimu. “Mbali na kutunga nyimbo mimi napiga ngoma na kupiga gitaa kidogo si sana, Mbalamwezi anapiga gitaa vizuri sana na Hamadai anapiga piano sana,” anasema Rhino King. HAMADAI Aliwahi kugonga vichwa vya habari za burudani alipokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Shilole, kuandika nyimbo za mastaa pamoja na nyimbo zake nje ya The Mafik kama vile Wangere, Marioo zilizofanya vizuri. “Nilipotakiwa kujiunga na The Mafik nilikuwa na furaha kwa sababu nilikuwa nawafahamu wenzangu, nilifurahi sababu timu ambayo nafanya nayo kazi inajiweza,” anasema. MBALAMWEZI Anasema jina hilo alilipenda baada ya kujua nguvu ya mwezi kwenye giza kitendo kinachoitwa mbalamwezi. “Nilikuwa sijui maana yake maana kabla nilishajiita majina mengi, nilipokuwa Mafia nilienda kuchukua samaki, muuzaji akaniambia wamepanda bei sababu ya mbalamwezi, akaniambia hawaonekani kwa sababu samaki ni ngumu kupatikana kwa sababu wanaona,” anasema. RHINO KING Anasema mbali na muziki ni mcheza soka katika dimba uwezo wake watu walimpa jina la Kifaru na alipoingia kwenye muziki akaamua kulitumia. “Niliitwa Kifaru wakati nacheza soka kwa sababu ya nguvu zangu, nikalitoa kwenye Kiswahili na kuliweka kwenye Kiingereza likaja Rhino nilipoanza rasmi muziki ili liwe na swag,” anasema. WALICHOJIFUNZA TAMASHA SAUTI ZA BUSARA The Mafik walikonga nyoyo za mashabiki wao visiwani Zanzibar katika tamasha kubwa la Sauti za Busara lililofanyika Februari 8-11 mwaka huu katika ngome za Mji Mkongwe. Je wawamepata uzoefu gani baada ya kutumbuiza kwenye tamasha hilo kubwa Afrika Mashariki? “The Mafik wapo kwenye familia kubwa, tukipata simu moja kwa moja kutoka kwa Fid Q kuwa The Mafik wanahitajika Zanzibar, sisi kama viongozi tukaona ni vizuri waende, ikawa hivyo ili wapate uzoefu kwenye majukwaa makubwa,” anasema Shetta. USO KWA USO NA BABU SEYA, PAPII OCHA The Mafik wanasema hii ni heshima kubwa kwao kupata nafasi ya kutumbuiza kwenye jukwaa moja na Babu Seya na Papii Kocha ikiwa ndiyo onyesho lao la kwanza linalotarajia kuhudhuliwa na mashabiki wengi. “Kama kawaida yetu sisi ni watu wa ‘live band’ kwa hiyo kesho (leo) pale jukwaani tumepanga tuandike historia ya aina yake kama kundi pekee linalotumbuiza na kina Papii Kocha na Babu Seya,” anasema Hamadai. PAPII KOCHA ATOA NENO “Hii ni shoo ambayo nilikuwa naiwaza kama ndoto hewa sababu nilikuwa sijui lini itatimia lakini kwa baraka za Mwenyezi Mungu na Rais Magufuli amefanya ndoto yangu iwe hai. “Mimi na mzee wangu tutakutana na ndugu jamaa na mashabiki zetu kesho (leo) kwa mara ya kwanza baada ya kutoonana nao kwa miaka 14,” anasema Papii alipozungumza na paparazi wa Swaggaz. | 1 |
MAKUBALIANO ya kimataifa yakiwemo yanayotaka Serikali kutoa kipaumbele kwa sekta kadhaa kwa kutenga kiwango fulani katika bajeti, yamebainika ni vigumu kutekelezwa ipasavyo kutokana na uhaba wa fedha zinazopaswa kugawanywa.Serikali imekiri kuhusu hilo ikisema kazi inayotakiwa kufanyika, ni kujielekeza kuwezesha ukusanyaji na kupata mapato zaidi ili vipaumbele vya kisekta na kitaifa viwekwe vizuri; vinginevyo nchi ikitekeleza maazimio kama inavyotakiwa, baadhi ya sekta zinaweza kukosa fedha.Miongoni mwa makubaliano ambayo serikali kupitia kwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango imekiri kwamba mbele ya safari inabidi kujipanga vizuri kabla ya kuyatekeleza, ni pamoja na Azimio la Sadc linalotaka serikali itenge asilimia 20 ya bajeti yote kwa ajili ya elimu.“Huko mbele tukifika, lazima tutapanga vizuri badala ya kusema tutatekeleza haya maazimio,” alisema Waziri Mpango wakati akijibu hoja za wabunge zinazohusu masuala ya fedha wakati wakichangia bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iliyopitishwa hivi karibuni.Katika maoni, mapendekezo na ushauri wa wabunge 116 waliochangia bajeti hiyo, baadhi yao walitaka serikali kuheshimu makubaliano ya kimataifa ikiwamo azimio hilo la SADC.Ingawa Dk Mpango alikiri kuwa serikali inapaswa kuyaheshimu, alisema licha ya azimio hilo la kutaka itengwe asilimia 20 ya bajeti yote kwa ajili ya elimu, yapo mengine yanayoelekeza utengaji wa sehemu ya bajeti kwa ajili ya sekta kadhaa.“Ni kweli; lakini yapo maazimio mengine ambayo Tanzania imekubali,” alisema Waziri Mpango na kutaja Azimio la Maputo sambamba na sekta na kiwango cha fedha kinachopaswa kutengwa kwenye bajeti.Kwa mujibu wa Dk Mpango, azimio hilo linataka serikali kutenga asilimia 10 ya bajeti yote kwa ajili ya kilimo; afya asilimia 15 ya bajeti yote; utafiti asilimia moja ya pato la taifa na asilimia 0.05 ya bajeti kwa ajili ya takwimu.“Sasa kama maazimio yote haya yatatekelezwa, sekta tatu tu zitachukua asilimia 45 ya bajeti yote. Sasa kipi kitasalia kwa ajili ya miundombinu, ulinzi na usalama, maji na bajeti ya bunge?” alisema Waziri Mpango.Waziri alisema ni muhimu wabunge wakazingatia kwamba pia sekta nyingine ni muhimu kwa maendeleo ya elimu.Alitoa mfano wa bajeti ya ulinzi na usalama kwamba ni muhimu kwani vijana walioko shuleni watasoma wakiwa wamehakikishiwa ulinzi na usalama.Vivyo hivyo kwa upande wa bajeti ya afya, maji, miundombinu ya umeme na teknolojia ya habari na mawasiliano. “Ni muhimu tuangalie mambo yote hayo, alisema na kusisitiza kwamba kikubwa ni ukubwa wa ‘keki’”.Alisema kazi inayotakiwa kufanyika ni kujielekeza kupata mapato zaidi ili vipaumbele vya kisekta na kitaifa viwekewe vizuri. Bunge linaendelea na mkutano wake wa bajeti jijini Dodoma ambako wizara kadhaa zimeshapitishiwa bajeti zake kwa mwaka 2019/20. Miongoni mwake ni Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambayo wabunge waliidhinisha na kupitisha bajeti ya Sh trilioni 1.3 kwa mwaka wa fedha 2019/20.Mwaka huu unaokaribia kumalizika (2018/19), wizara hii ilitengewa Sh trilioni 1.4 kiasi ambacho kwa kulinganisha na bajeti ijayo, wabunge walitafsiri kuwa bajeti ya elimu imeshuka.Akizungumzia tafsiri kwamba bajeti ya elimu imeshuka na kwamba bajeti ya maendeleo imekuwa na mserereko wa kupungua, Dk Mpango alisema kwa kuangalia takwimu, ni kweli.Alisema, “ukiangalia takwimu, zinaonesha bajeti inapungua katika kutoka asilimia 17 ya bajeti yote 2015/16; asilimia 16 mwaka 2016/17 asilimia 15 mwaka 2017/18 asilimia 14 mwaka 2018/19 na asilimia 14 ya mwaka ujao wa fedha.“Hata hivyo, si kweli kwamba bajeti ya maendeleo imekuwa na mserereko wa kupungua. Ukiunganisha hizi namba unaona kilichopungua ni bajeti ya matumizi ya kawaida na inapungua kwa miaka miwili iliyopita,” anasema.Anaainisha mwaka 2015/16 bajeti ilikuwa Sh bilioni 3.2 ikaongezeka hadi Sh bilioni 3.7 kwa mwaka 2016/17. Mwaka 2017/18 ndipo ilishuka kidogo hadi Sh bilioni 3.5 na mwaka huu ni Sh bilioni 3.4 huku kwa mwaka ujao (2019/20) ikishuka hadi Sh bilioni 3.1.Hata hivyo, alisema hali hiyo inatokana na hatua ambazo serikali ilichukua ikiwamo kuondoa watumishi hewa kutoka katika sekta ya elimu na pia uundaji mpya uliofanyika katika taasisi mbalimbali na kuondoa baadhi ya watumishi kutoka kwenye taasisi mbalimbali za wizara.Waziri alisema ni muhimu wabunge wakatambua mchango mkubwa wa wadau wengine wa elimu nchini na hususani wamiliki wa shule binafsi lakini pia taasisi za dini. | 3 |
BERLIN, Ujerumani SERIKALI ya hapa imesema ina matumaini ya kufanyika uchaguzi
huru nchini Sudan na imeuwasilisha mgogoro wa nchi hiyo kwenye Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa (UN). Hata hivyo serikali
hiyo imesisitiza kuwa Omar al-Bashir afikishwe kwenye mahakama ya kimataifa ya
Uhalifu wa Kivita (ICC). Katika mkutano na
waandishi wa habari, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Christopher Burger
aliweka tahadhari wakati alipoisoma taarifa rasmi juu ya hali inayobadilika kwa
haraka na isiyotabirika ya nchini Sudan. Msemaji huyo alisema
jambo la uhakika ni kwamba Aprili 11 mwaka huu, jeshi katika jiji la Khartoum
lilichukua udhibiti wa kituo cha televisheni cha taifa na kutangaza litatoa
tamko baadaye juu ya hali ya kisiasa ya Sudan na na kwamba Rais wa muda mrefu
Omar al-Bashir ameondolewa madarakani. Hata hivyo, watu
wengi waliingia mabarabarani mwishoni mwa wiki usiku ili kuendelea kuonyesha kwamba wanataka jamii
huru, demokrasia na nchi itayoongozwa na serikali ya kiraia. Msemaji huyo alitoa
wito kwa pande zote zijizuie kwa sababu ufumbuzi wa amani katika mgogoro huo
unahitajika na pia utakaozingatia matarajio ya watu wa Sudan wanaotaka
mabadiliko. Burger alisema
Ujerumani, ambayo mwezi huu inashikilia urais wa zamu wa Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa, imeupa kipaumbele mgogoro wa Sudan kati ya ya ajenda zitakazojadiliwa
pamoja na washirika wake wa Ulaya na Marekani. Alhamisi wiki
iliyopita, Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa tahadhari juu ya hali katika nchi hiyo
ya Mashariki mwa Afrika na iliandikwa kwenye tovuti yake kwamba Usafiri wote
usio muhimu kwenda nchini Sudan unapaswa kuepukwa, na viwanja vya ndege na
mipaka kwa sasa imefungwa. Mpaka sasa haijulikani
bado alipo Rais Al Bashir lakini msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ameeleza kuwa
msimamo wa Ujerumani upo wazi kwamba hati ya kukamatwa kwa kiongozi huyo iliyotolewa na ICC kwa madai ya uhalifu dhidi
ya binadamu, uhalifu wa kivita na mauaji ya kimbari katika jimbo la Darfur bado
ina nguvu. Rais Bashir mwenye
umri wa miaka 75 anatuhumiwa kwa kuwatumia askari na jeshi lake kuyasakama
kikatili makundi ya wachache huko Darfur Magharibi mwa Sudan mnamo mwaka 2003. Inakadiriwa watu
300,000 waliuawa katika vita hivyo. Uongozi mpya wa kijeshi wa nchini Sudan
umesema al-Bashir atafunguliwa mashtaka nchini na siyo nje ya Sudan. | 2 |
OFISI ya Uhamiaji kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama Mkoa wa Pwani wamekamata wahamiaji haramu 12 kutoka nchi za Ethiopia na Somalia.Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama akizungumza na waandishi wa habari amesema wahamiaji hao walikuwa wamejificha porini.Ndikilo amesema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 7, mwaka huu eneo la Darajani kwenye pori la Ranchi ya Ruvu katika Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo.“Wahamiaji hao haramu ambao 11 wanatoka nchi ya Ethiopia na mmoja Somalia walikuwa wamejificha katikati ya pori hilo na walikamatwa na wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi ambao walikuwa kwenye mafunzo kwa kushirikiana na Uhamiaji na Jeshi la Polisi,” amesema Ndikilo.Alisema kuwa pia walifanikiwa kuwakamata Watanzania wawili ambao walikuwa wakiwapelekea chakula wahamiaji hao huku mmoja akikimbia licha ya askari kufyatua risasi juu ili asimame bila ya mafanikio.“Vyombo vyetu tayari vimeshamfuatilia mtu aliyekimbia na wameshapata namba yake ya simu na mahali anapoishi ambapo ni Mlandizi sehemu inayoonekana kushiriki sana kwenye suala la kuwahifadhi na kuwasafirisha wahamiaji haramu,” alisema Ndikilo.Aidha alisema wanashangaa ni kwa nini wahamiaji hao haramu hukaa huko na kuonesha wasiwasi kuwa yawezekana ni wahalifu au watu hatari kwa nchi. “Tunawataka wale wanaosafirisha au kuwatunza waache na kama baadhi ya wanaotoka vyombo vya dola waache kwani hatua kali zitachukuliwa.”Msimamizi na Mdhibiti wa Mipaka wa Uhamiaji Mkoa wa Pwani, Abtwalibu Yusuf amesema, baadhi ya wahamiaji haramu hutumia njia ya maji.Pwani ina bandari bubu zaidi ya 30.Yusuf amesema katika kudhibiti uingiaji haramu wa watu hao wamekuwa wakishirikiana na vyombo vingine vya usalama vya wilaya pia kwa upande wa njia ya barabara wanashirikiana na polisi na wasamaria wema.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Barnabas Mwakalukwa alisema kuwa wananchi wanapaswa wasijihusishe na kuwahifadhi au kuwasafirisha wahamiaji haramu na kutoa huduma yoyote kwani ni kosa la jinai na wanapowaona watoe taarifa kwenye vyombo vya dola. | 3 |
Na RAMADHANI MASENGA
NIAJE wanangu? Mambo ni nini? Masela mwanenu bado buku tu niwe milionea. Hamuamini? Shauri zenu. Niungieni buku mwanenu niwe tajiri namba tatu Tanzania.
Hakika laifu ni mikakati. Bila mikakati na mipango makini hutoboi. Saa mwananenu naelekea kutoboa. Kila mmoja wenu akinichangia buku nami nakuwa milionea.
Nimepigika sana na laifu la Kibongo. Nimesuka sana mipango. Nimekesha nikitafuta mbinu za kitajiri. Sasa baada ya kuhangaika kwa mingomingo nimepata siri. Buku tu itanifanya niwe tajiri namba tatu Tanzania.
Masela nichangieni. Bila kusaidiana hii laifu hatutoboi. Inatajwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ya uchumi wa Tanzania unashikiliwa na watu wenye asilia ya kiasia (hasa hawa akina vevee).
Cha kushangaza hawa watu wako asilimia kama 20 tu katika taifa letu. Unajua siri ya kutoboa kwao? Kusaidiana. Hawa watu wanabebana kinoma noma.
Wakimuona mwenzao kakwama, lazima wampige tafu. Sasa wanangu katika mambo mukide kama haya kuigana lazima.
Kama akina cholicholi wanavyopigana tafu, basi msiache kunipiga tafu na mimi mwanenu wa faida. Nichangieni buku niwe milionea masela.
Nimepigika sana katika hili laifu. Nimepata visenti kadhaa nikaishia kuhonga na kubeti. Nimetumikishwa miaka kibao bila mafanikio ya maana.
Kwa siri hii, sitakuwa mtumwa tena wanangu. Nipeni buku nipate utajiri. Kwa miaka zaidi ya kumi nilidhani ili niwe na mijihela ni lazima nirithi mabasi au visima vya mafuta kama watoto wa Kiarabu.
Kwa fikra hizo, kila senti yangu ikaishia kwenye bata na pochi za mademu kwa sababu niliona haitoshi. Sasa nimegundua uchawi wa maisha yangu ni nini.
Mkiniongezea buku tu na mimi natusua. Nakuwa mzito, bosi, milionea. Kila demu aliyenitosa atanifuata na kutaka upya namba yangu ya simu.
Mnajiuliza ni kwanini buku? Basi ngoja niwachane. Kila safari ndefu huanza na hatua chache. Ili ufikie milioni mia, basi unatakiwa uwe na nidhamu ya kutunza pesa ndogo unayopata.
Kwa maana hiyo, ukiwa na uwezo wa kuifanya buku kuwa buku tano ama kumi, basi una uweo wa kuifanya buku kumi kuwa laki. Kwa mtindo huo unaukaribia umilionea bila tabu.
Umegundua nini hapo? Acha uboya. Usilalamike kuwa laifu ni taiti wakati huna nidhamu ya fedha. Unanunua sigara ngapi kwa siku?
Pakti mbili kisha baadaye unalalamika huna hela ya kula. Unatumia kiasi gani kwenye ulabu? Halafu kesho yake unalalama maisha magumu! Oya vipi mwanangu? Acha kuzingua pimbi wewe.
Nishakisanua asa utaamua mwenyewe kujiongeza au uendelee kumbwela. Wenzio tushaachana na mambo ya kupiga vizinga, tunameki ndogondogo daadeki. Nduki kwa sana! | 1 |
KATIKA kuhakikisha jamii ya Watanzania inakuwa salama kiafya kutokana na bidhaa mbalimbali wanazonunua kwa mahitaji yao, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linaendelea na kampeni yake ya kudhibiti bidhaa zisizo salama ikiwa ni pamoja na mitumba hatarishi, hususani nguo za ndani.Kwa mujibu wa TBS nguo za aina hiyo, zinazoweza kuuzwa katika maeneo mbalimbali nchini hazina ubora unaotakiwa kwa matumizi ya mwanadamu. Ni kwa mantiki hiyo, TBS imekuwa ikifanya ukaguzi wa kushitukiza ili kuhakikisha wafanyabiashara wachache hawaendelei kuuza bidhaa hizo hatarishi.Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora wa TBS, Lazaro Msasalaga, anasema pamoja na kufanya ukaguzi, hususani kwa wafanyabiashara ndogo wanaouza nguo hizo za ndani za mitumba, wamekuwa wakiwaelimisha juu ya madhara ya kiafya ya kuuza nguo hizo na kwamba kuziuza ni kinyume cha sheria. Mitumba isiyotakiwa kuuzwa Ofisa Viwango Mwandamizi wa TBS, Paulo Manyilika anasema kiwango elekezi cha taifa cha nguo za mitumba (TZS 758:2017), toleo la tatu, kinapiga marufuku kuagiza nguo za ndani za mitumba na zile zinazotumika kukaushia mwili.“Pia kinapiga marufuku ya kuagiza nguo ambazo hazikufukizwa dawa za kuzuia magonjwa ambukizi kwa mujibu wa sheria,” anasema. Manyilika, anasema kiwangoelekezi hicho kinazitambua nguo za ndani zilizopigwa marufuku kuwa ni pamoja na chupi, sidiria, boksa, soksi na fulana za ndani.Anaongeza aina ya nguo zingine za mitumba zinazopigwa marufuku kuuzwa ni zile zinazotumika kukaushia mwili ambazo ni mataulo ya bafuni, mezani, chooni na leso za mikononi. Madhara kiafya Anasema nguo ambazo hazikufukizwa dawa ili baadaye ziweze kutumika kwa ajili ya matumizi ya binadamu, zinaweza zikasababisha madhara ya magonjwa ya ukoma, ngozi, kifua kikuu, kimeta, uti wa mgongo, kipindupindu na ugonjwa wa ebola.“Ni vyema wafanyabiashara ndogo wanaouza nguo hizi, wakiziona kwa wafanyabiashara wa jumla watoe taarifa kwetu ili tuweze kuchukua hatua,” anasisitiza. Anasema pamoja na kwamba mitumba inapaswa kuwa imefukizwa dawa, hii haizuii mtumiaji kuathirika kwa kuwa, uwezekano wa mabaki ya vimelea ambukizi kwenye mitumba upo hasa kwa mazingira ya nguo zinazopigwa marufuku.Anazidi kufafanua kwamba dawa zilizofukiziwa pia zinaweza kumdhuru mtumiaji kwani nguo za ndani zinavaliwa kwenye maeneo ambayo hugusana na ngozi kwa muda mrefu. “Nguo hizi zinavaliwa kwenye maeneo ambayo hutoka jasho na yenye ngozi laini kwa hiyo ni rahisi kumwambukiza mtumiaji,” anasema.Anasema wanaopuuza maelekezo hayo ya TBS wanaweza kupata maambukizi ya fangasi, magonjwa ya ngozi (tropical diseases) na saratani ya ngozi. Msasalaga anasema TBS imefanya kazi kubwa ya ukaguzi ili kuhakikisha kuwa watumiaji wa bidhaa mbalimbali nchini wanatumia bidhaa bora na sio bidhaa dhaifu ambazo zinaingizwa kwenye masoko ya hapa nchini.Kwa upande wa nguo za ndani za mitumba ambazo hazina ubora, anasema TBS ambayo kwa sasa inaendelea na ukaguzi kwa nchi nzima, imeshakamata jumla ya tani 3.5 za nguo za mitumba ambazo hazina ubora na zisizofaa kwa matumizi ya binadamu. Anasema nguo hizo zenye thamani ya Sh milioni 42 zimekamatwa katika masoko ya mikoa ya Mara, Shinyanga na Dar es Salaam kati ya Januari hadi Aprili mwaka huu.Anafafanua kwamba nguo kiasi cha tani mbili zenye thamani ya Sh milioni 12 kilikamatwa katika soko la jiji la Dar es Salaam na kiasi cha tani moja na nusu chenye thamani ya Sh milioni 30 kilikamatwa katika masoko ya kanda ya Ziwa. Anasema nguo hizo tayari zimeharibiwa. Anasema wamekamata pia shehena tani tano za biskuti katika jiji la Mwanza ambazo zimeingizwa jijini humo zikitokea nchi jirani, zenye thamani ya Sh milioni 40 huku zikiwa hazina ubora.“Kiasi cha marobota 13 ya mitumba tumeyakamata katika soko la Musoma mkoani Mara na kuyateketeza baada ya kubainika kutokuwa na ubora kwa ajili ya matumizi ya binadamu,” anasema. Anawataka wananchi hususani wafanyabiashara wa nguo za mitumba kutambua kuwa yako madhara makubwa ya kiafya kwa mtu anayevaa nguo za mitumba za ndani. “Tumeteketeza nguo hizo kwa mujibu pia wa kiwango cha ubora cha kimataifa (ISO) cha 758.17 kinachokataza matumizi ya nguo za ndani zilizokwishatumika kuuzwa kwa watu wengine,” anasema.Anawataka wafanyabiashara wa mitumba kuwa mabalozi wema na waache kununua nguo za mitumba za ndani kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa na badala yake watoe taarifa za uwepo wa bidhaa za nguo zilizopigwa marufuku kwenye mamlaka za serikali ikiwemo TBS na polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe. “Mfanyabiashara wa jumla wa nguo za mitumba, atakayebainika kukiuka utaratibu huu uliowekwa na serikali atachukuliwa hatua zitakazomsababisha kujutia kosa lake, hakutakuwa na huruma,” anasema.Ofisa Masoko wa TBS, Debora Haule anasema TBS itaendelea na ukaguzi na kutoa elimu kwa jamii kupitia radio za kijamii, hasa maeneo ya vijijini ambako kuna watu wasiopata taarifa za kutosha kwa wakati. Anasema katika kudhibiti nguo za mitumba ambazo hazina ubora kwenye soko, TBS itaendelea kutoa elimu kwa umma nchini kote juu ya umuhimu wa kudhibiti nguo hatarishi za mitumba na bidhaa zingine ambazo hazina ubora.Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa TBS Kanda ya Ziwa, Evarist Mrema anasema TBS itaendelea na udhibiti wa bidhaa za nguo ambazo hazina ubora kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa. “Sanjari na udhibiti wa ubora, tutaendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya kutumia bidhaa hafifu zilizo sokoni. Ninawaomba watembelee ofisi yetu ya Kanda watakapokuwa na tatizo,” anahitimisha Mrema.TBS ni Shirika la Umma lililo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara lililoundwa kwa mujibu wa sheria ya bunge namba 3 ya mwaka 1975. Baadhi ya majukumu ya TBS ni pamoja na kuandaa viwango katika sekta zote za uchumi, huduma na biashara, kuvisimamia na kuvitangaza viwango vya kitaifa, kusimamia utekelezaji wa matumizi ya viwango kupitia kwa watumiaji na kusimamia ubora wa bidhaa zinazozalishwa ama kuingizwa nchini ama kusafirishwa nbje ya nchi.Katibu wa Jumuiya ya Wamachinga Wilaya ya Nyamagana, Hidaya Juma anakiri kwamba wananchi wengi wanakimbilia nguo za mitumba kwa sababu ya bei yake kuwa nafuu na uimara wake, lakini anasema ameelimika kuhusu elimu inayoendelea kutolewa kwani hata yye bi mbaji mkubwa wa mitumba. | 3 |
MOSCOW, Urusi RAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amesema kwamba, Serikali yake inaunga mkono kwa dhati wazo la kuanzisha soko huru katika nchini za Bara la Asia na Pasifiki. Rais Putin alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki kupitia taarifa yake iliyotolewa na Wizara ya Habari nchini hapa na kusambazwa katika vyombo mbalimbali vya habari. Katika taarifa hiyo, Rais Putin, alisema kwamba kwa kuanzishwa soko hilo kutachochea maendeleo ya haraka kibiashara baina ya nchi hizo zilizopo katika ukanda huo wa Asia na Pasifiki. “Tunaunga mkono kwa dhati wazo la kuanzishwa soko huru kwa nchi za bara la Asia na Pasifiki,” ilieleza taarifa hiyo iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari nchini hapa. “Tunaamini kwamba, hatua hii ni kwa ajili ya manufaa yetu na inaonyesha fursa ya kuimarisha nafasi zetu katika masoko ya APR ambayo yanakuwa kwa kasi. Nataka kutambua kwamba zaidi ya miaka mitano iliyopita, sehemu ya uchumi wa APEC katika biashara ya nje ya Urusi imeongezeka kutoka asilimia 23 hadi 31 na kutoka asilimia 17 hadi 24 katika mauzo ya nje. Na hatuna nia ya kuishia hapo,” iliongeza taarifa hiyo. Akiunga mkono zaidi hatua hiyo, Rais Putin, alisema mradi huu utakaoanzishwa unapaswa kutekelezwa kwa sababu ya uzoefu wa muundo muhimu wa ushirikiano katika nchi za Asia, Pasifiki na Eurasia, hasa Umoja wa Kiuchumi wa Eurasian (EEU) ambapo Urusi inashirikiana na Armenia, Belarus, Kazakhstan na Kyrgyzstan. Alisema umoja wao umeendelea kuimarika kwa nguvu na akasema kuwa wanatamani kujenga uhusiano na nchi zote na vyama ambavyo vina nia ya kufanya hivyo. | 2 |
UJENZI wa mabweni mengi ya wasichana pamoja na sekondari nyingi nchini ni kati ya sababu zilizochangia serikali kuwachukua wanafunzi wa kike wote waliofaulu kujiunga na kidato cha tano mwaka huu. Juzi Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), ilitangaza kuwachukua wanafunzi wote wa kike wenye sifa za kujiunga na kidato cha tano na elimu ya ufundi. Tukio hilo ambalo ni mara ya kwanza kuwahi kutokea nchini, limesababisha wanafunzi 108,644 sawa na asilimia 98.31 ya wanafunzi 110,505 wenye sifa waliotangazwa kuchaguliwa mwaka huu kujiunga na kidato cha tano. HabariLeo imezungumza na Naibu Katibu Mkuu Tamisemi anayeshughulikia elimu, Tixon Nzunda ambaye alibainisha kuwa sababu kubwa ya mafanikio hayo ni ujenzi wa mabweni ya wasichana pamoja na sekondari za kutwa nyingi sehemu mbalimbali za nchi. Nzunda alibainisha kuwa serikali imepeleka zaidi ya Sh bilioni 29 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na mabweni mikoa mbalimbali nchini kipindi cha kuanzia Januari mwaka huu. Alisema, kumekuwa na ongezeko kubwa la ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi wa sekondari ambapo mengi ni mabweni ya wasichana, hali ambayo imechangia kuchukuliwa kwa wasichana hao wote kwenye matokeo ya kidato cha tano mwaka huu. Alisema,”mabweni mengi yamejengwa pamoja na shule za sekondari za kutwa, hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kuchukuliwa kwa wasichana wote waliofaulu kidato cha tano mwaka huu. Lakini pia ifahamike kuwa kuna sera ya kuwawezesha wasichana kupata elimu ya juu zaidi ila hiyo sio sababu kubwa ya wao kuchukuliwa kwa maana ya hatujawapendelea wao tu na kuwaacha wanafunzi wa kiume”.Alisema wanafunzi wa kiume walioachwa ambao ni 1,861 watachukuliwa wote kwenye udahili wa awamu ya pili. Alisema Tamisemi kupitia mikoa mbalimbali imefanikiwa kujenga madarasa takribani 2,093 nchi nzima kwa gharama ya Sh bilioni 29.9. Kwa upande wa shule za msingi imejenga madarasa 2,897 kwa gharama ya Sh bilioni 35 huku akibainisha kuwa miundombinu ya kuwawezesha wanafunzi wa shule za msingi kusoma vema ili kujiunga kwa wingi sekondari inazidi kuboreshwa. Juzi Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo alibainisha kuwa wanafunzi 108,644 sawa na asilimia 98.31, ya wanafunzi 110,505 wenye sifa, wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo mbalimbali vya ufundi nchini.Jafo alifafanua kuwa jumla ya wanafunzi 69,356 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano ambapo katika chaguo hilo, idadi ya wasichana ni 31,809 na wavulana 37,547 sawa na asilimia 62.76 ya wanafunzi 110,505 ya waliokuwa na sifa. “Waliojiunga na shule za wanafunzi wenye ufaulu mzuri zaidi (vipaji maalumu) ni 1,462 ambapo wasichana ni 646 na wavulana 816. #Miongoni mwao wanafunzi sita ni wenye mahitaji maalumu ambao wasichana ni watatu na wavulana watatu,” alisema. Aliongeza kwamba wanafunzi wenye mahitaji maalumu waliochaguliwa ni 157 ikiwa wasichana ni 74 na wavulana ni 86 wakati wanafunzi waliochaguliwa ambao waliosoma chini ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima ni 174, ikiwa ni wasichana 74 na wavulana 100. Aidha, Jafo alisema wanafunzi 1,046 ikiwa ni wasichana 257 na wavulana 789 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vinne vya Elimu ya Ufundi ambavyo ni Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Chuo cha Usimamizi wa Maendeleo ya Maji (WDMI) na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST). Jafo pia alisema wanafunzi 32,619 ikiwa ni wasichana 11,665 na wavulana 20,954 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vingine vya elimu ya ufundi vinavyosimamiwa na NACTE. Akichanganua waliochaguliwa na idadi yao kwenye mabano kuwa ni waliochaguliwa vyuo vya afya kwa astashahada 345 na stashahada ni 1,477, vyuo vya walimu ni 4,472 wa astashahada na 4,146 wa stashahada. Jafo alisema Vyuo vya Ardhi ni wanafunzi 464, Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo (2,850), Chuo cha taifa cha Utalii (450), Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (1,500), Chuo cha Mipango-Dodoma (2,200), Chuo cha Usimamizi wa Fedha (1,864), Vyuo vya Uvuvi-FETA(575), vyuo vya mafunzo ya kilimo-MATI (921), Taasisi ya Uhasibu Arusha-IAA(1,295). Vyuo vya Maendeleo ya jamii-CDTI (1,573), Taasisi ya Uhasibu Tanzania- TIA(5,254), Vyuo vya Mafunzi ya Mifugo-LITA (1,281), Vyuo vya utumishi wa Umma-TPSC( 3,955) na Chuo cha Elimu ya Biashara-CBE( 3,620).Aidha, Jafo ameagiza wanafunzi wote waliopangiwa kujiunga kidato cha tano wanapaswa kuripoti katika shule walizochaguliwa ndani ya siku 14 kuanzia Julai 8 mwaka huu na baada ya muda huo kupita nafasi itachukuliwa na wanafuzni mwingine aliyekosa nafasi. “ Mabadiliko ya shule yataruhusiwa baada ya kukamilika kwa muhula wa kwanza wa masomo na utaratibu huo utafanyika kwa kuzingatia uwepo wa nafasi kwenye shule kwa idhini ya maafisa elimu wa mikoa husika,” alisema. | 3 |
Upendo Mosha – Moshi Uongozi wa soko kuu la mitumba la Memorial, Manispaa ya Moshi Mkoani
Kilimanjaro, umeahidi kushirikiana na jeshi la Polisi kupiga marufuku
wafanyabiashara wa soko hilo kwenda sokoni hapo na watoto wenye umri chini ya
miaka mitano. Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa soko hilo, Godfrey Shayo, leo
Juni 24, wakati wa utafiti wa kuongeza uelewa, uwajibikaji wa huduma bora za
malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto (ECD), zoezi linalo tekelezwa na muungano
wa vilabu vya waandishi wa habari nchini (UTPC) kwa kushirikiana na
taasisi ya CIC ya Ireland “Ukija sokoni hapa majira ya saa 11 Alfajiri utaona wazazi na walezi
wakiwa na watoto wachanga huu ni ukatili na unaathiri afya ya mtoto na malezi
yake ya baadaye, tumeliona hili na tunaandaa mpango wa kutoa elimu kabla ya
kuchukua hatua” amesema. Kwa upande wake mwenyekiti wa masoko la Mbuyuni, Lameck
Mziray na mwenyekiti mtaa wa soko la Pasua, Rahibu Juma walikiri kuwapo kwa
changamoto inayoathiri afya za watoto hao lakini wameahidi kuandaa mpango wa
ushirikishwaji na wafanyabiashara ili kujadili suala hilo. Naye Daktari bingwa mwandamizi wa afya ya jamii, Uzazi na
magonjwa ya akina mama, Dk Moke Magoma amesema malezi hayo yasipothibitiwa
yatachangia kwa asilimia kubwa kujenga taifa la kizazi kisicho na mwelekeo na
chenye urahisi wa kujihusisha na matukio ya uhalifu. Aidha kabla ya kufanyika kwa zoezi hilo, uongozi huo utatoa
elimu kwa wazazi na walezi wenye watoto kuanzia miaka sifuri hadi mitano
ambao wanaonekana sokoni hapo kuanzia saa 12 alfajiri hadi saa moja usiku
wakiwa na wazazi wao. | 3 |
RAYMOND MINJA IRINGA Idara ya
Uhamiaji mkoni Iringa inawashikilia watuhumiwa 20 wa makosa ya kiuhamiaji ambao
19 ni raia wa Kenya wenye asili ya Somalia na raia 1 wa Tanzania. Akizungumza
na vyombo vya habari Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishina Msaidizi
Mwandamizi wa Uhamiaji SACI, Agnes Michael Luziga amesema watuhumiwa hao
wameingia nchini kinyume na sheria ya uhamiaji Sura ya 54 Rejeo la mwaka 2016
(Immigration Act Cap 54 RE 2016)na kanuni zake. Amesema
watuhumiwa hao wamekamatwa mapema wiki hii katika maeneo ya Mtera getini mkoani
Iringa mara baada ya kikosi cha doria cha uhamiaji kupata taarifa za
kiintelejensia kutoka kwa askari wa SUMAJKT Kituo cha mtera. Aidha
ametoa wito kwa Watanzania kuiga mfano kwa kuwafichua wahalifu wa aina hiyo
kwani jukumu la ulinzi na usalama wa taifa
na mipaka yake ni la kila mtanzania. Katika zoezi la kupambana na wahamiaji haramu Idara ya uhamiaji
Tanzania inaendelea kutoa elimu kwa umma kwa njia ya televisheni, redio, magazeti,
mikutano ya hadhara na mitandao ya kijamii ili kuwahasa wananchi kushiriki kwa
kutoa taarifa uhamiaji pindi wanapokutanana na mtu au au kundi la watu ambao
wanawatilia mashaka katika maeneo yao ya kazi ili kuwezesha idara kuchunguza na
kubaini sababu za ujio wao na shughuli zao hapa nchini. | 3 |
Na JUDITH NYANGE,
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella jana alilazimika kuvunja kikao cha wadau wa elimu wa mkoa baada ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, maofisa elimu wa msingi na sekondari kutoka baadhi ya halmashauri kutohudhuria.
Kikao hicho cha wadau wa elimu Mkoa wa Mwanza kilipangwa kufanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi kujadili hali halisi ya elimu.
Mambo mengine ni changamoto zinazoikabili sekta hiyo na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zilizopo na barua za mwaliko wa kikao hicho zilitolewa miezi miwili iliyopita.
Lakini hadi saa 3:18 asubuhi wakurugenzi wote wa halmashauri za wilaya za mkoa huo walikuwa hawajawasili katika ukumbi wa mikutano.
Mongella ambaye alikuwa ndiye mwenyekiti wa kikao hicho alisema ana taarifa ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga, aliyekwenda kushughulikia mgogoro wa ardhi na si wengine.
Hata hivyo aligundua kutoalikwa kwa wadau muhimu katika kikao hicho kikiwamo Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Mwanza, Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSA) mkoa.
Alisema wakurugenzi wengi hawakuwapo wakati maofisa elimu ya msingi na sekondari walituma wawakilishi katika kikao hicho.
Mpaka saa 3:20 asubuhi viongozi wa wilaya waliokuwapo ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Dk. Leornard Masale, Mkuu wa Wilaya ya Magu, Hadija Nyembo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba, Pendo Malabeja, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa, Crispin Luanda na baadhi ya maofisa elimu msingi na sekondari. | 3 |
Na Mwandishi Wetu KATIKA jitihada za kuwezesha wajasiriamali na wakulima mkoani Geita, mgodi wa dhahabu Geita (GGML), umetumia zaidi ya Sh milioni 330 kujenga ghala la kisasa lenye uwezo wa kuhifadhi tani 30,000 ili kuwezesha wakulima kuhifadhi zao la mpunga. Hii yote ni moja ya sehemu ya jitihada za GGML kunufaisha jamii inayowazunguka kupitia Mpango wa Maendeleo ya Uchumi Mkoa wa Geita (Geita Economic Development Project – GEDP). Mpango huo unahusisha pia kilimo cha alizeti, ushonaji nguo na kudarizi, uchomeleaji (welding), utengenezaji viatu (shoe making) na ufyatuaji tofali za kisasa (Interlocking blocks), unalenga kuwezesha wananchi kiuchumi. Tatizo la kuharibika mazao kwa kukosa soko au kuuza bei ya chini ili yasiharibike, imekuwa ni changamoto kubwa kwa wakulima Tanzania na hata Mkoa wa Geita. Ujenzi wa ghala hilo, unakwenda sambamba na uwezeshwaji wa wakulima kupata mavuno kwa wingi zaidi ya awali, baada ya GGM kupeleka watafiti wa kilimo kutoka Taasisi ya Kilimo CHOLIMA ya mkoani Morogoro na kuwapatia elimu ya ukulima wa kisasa. Wakulima walikuwa wanavuna magunia tisa kwa heka, lakini sasa wanavuna 35 – 40 kwa heka, imekuwa lazima kuwezesha mfumo mzima wa zao ili kunufaisha wananchi. Akizungumzia ghala hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Saragulwa na kiongozi wa Chama cha Ushirika kinachojumuisha vijiji vya Nyansalwa, Bugulula, Salagulwa, Kasota na Manga (NYABUSAKAMA Agriculture Marketing Cooperative Society Ltd), Yuda Ng’hindi, anasema ghala hilo ni msaada mkubwa kwa wakulima. “Tunaishukuru Kampuni ya Geita Gold Mine Ltd kutujengea ghala kubwa la kisasa. Kukamilika kwake ni msaada mkubwa, tunakuwa na uhakika wa kuhifadhi mavuno yetu na kuyauza kwa wakati mwafaka,” alisema Ng’hindi. Naye Meneja wa Mawasiliano na Mahusiano wa GGML, Tenga B. Tenga, amesema kampuni yake itaendelea kusaidia miradi endelevu yenye kuleta tija kwa jamii ya Geita na Tanzania kwa ujumla. “Mradi huu, ni mojawapo tu ya juhudi kubwa tunayoifanya ili kuleta tija kwa wakulima na wakazi wa mkoa huu. GGM itaendelea kuwa chachu kubwa ya maendeleo kwa wadau na kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania,” anasema Tenga. Anasema ghala hilo, Kampuni ya GGML pia imewezesha ulimaji wa heka 900, upandaji na ununuzi wa mbolea. Hii ni pamoja na ununuzi wa trekta jipya na kupeleka wataalamu wa kilimo ili kutekeleza kilimo cha kisasa kitakachokuwa na manufaa hata baada ya kampuni ikapomaliza shughuli zake mkoani Geita. | 3 |
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Januari Makamba amesema serikali haipendi kuona wananchi wanapigwa na kunyanyaswa wakati wa utekelezaji kanuni za kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki hapa nchini.Januari aliyasema hayo wakati alipozungumza na wakuu wa mikoa na makatibu tawala wa mikoa kutoka mikoa 26 waliokutana jijini hapa kupitia na kujadili mambo mbalimbali.Alisema serikali imefikia uamuzi wa kupiga maru- fuku matumizi ya mifuko ya plastiki baada ya nchi nyingi duniani kukubaliana kufanya hivyo kutokana na tafiti kubainisha madhara ya mifuko ya plastiki katika mazingira ambapo wastani wa mfuko kuoza ni miaka 400 hadi 1,000.Januari alisema katika kutekeleza hilo, serikali imekuja na kanuni ambazo zitasimamia utekelezaji wa katazo za matumizi ya mifuko ya plastiki na kusisitiza haja ya kulitekeleza hilo kwa amani bila kuleta bughudha kwa wananchi. “Ambacho hakitapendeza kuonekana, ni kuonekana tunakimbizana na wananchi, tunapigana virungu, tun- abughudhi watu.Hatutegemei hili jambo likawa jambo la hovyo ambapo watu wanavunjwa mikono na baadaye jambo hili likaharibika na kutuharibia nchi na hasa chama tawala kikapakwa matope,” alieleza.Alisema ni vyema jambo hilo likatekelezwa kwa njia ya amani na kuijengea sifa nchi na serikali duniani kote. “Kuna nchi 60 duniani zilitangaza kupiga maru- fuku matumizi ya mifuko ya plastiki lakini nchi nyingi zilijaribu na kushindwa kwas ababu ya kushindwa kujipanga na maslahi ya wazalishaji wa mifuko ya plastiki kuingiza kwenye siasa za nchi,” alisema.Alisema serikali imejipanga kulitekeleza jambo hilo katika hali ya amani hasa baada ya kuendelea kutoa elimu kwa umma na kutengeneza upungufu wa mifuko ya plastiki kwenye mzunguko kwa kutumia njia mbalimbali ili isiwe shida utakapofikia utekelezaji wa kanuni hizo. Aidha, Januari alisema wakuu wa mikoa na makatibu tawala wa mikoa wana wajibu mkubwa katika kusimamia utekelezwaji wa kanuni hizo.“Hivyo tunaomba ushirikiano wenu, tunafahamu mkisimamia jambo kama wakuu wa mikoa na makatibu tawala wa mikoa linafanikiwa kwani kuna mfano mingi ya mafanikio ya ushiriki wenu.Kuhusu hoja ya kuwa katazo hilo litachangia ukosefu wa ajira, Januari alisema kuwa suala hilo limefanyiwa utafiti na kuwa mifuko mbadala itatoa ajira zaidi kwa Watanzania kuliko ilivyo sasa ambapo asilimia 80 ya mifuko hiyo inatoka nje ya Tanzania.“ Niwatoe hofu ya kupotea kwa ajira, ukweli ni kwamba viwanda zinavyozalisha mifuko ya plastiki pekee ni vichache, wazalishaji wa vikapu na mifuko mbadala watakuwa ni wengi kuliko walioajiriwa kwenye viwanda. Pia asilimia 80 ya mifuko inazalishwa nje ya Tanzania, hivyo kuendelea kuchelewa kuizuia kwa hoja ya kulinda viwanda, tafsfiri yake ilikuwa ni kulinda viwanda vya nje. | 3 |
NA THERESIA GAPER, DAR ES SALAAM MSHAMBULIAJI wa Simba, Hamis Kiiza ‘Diego’, ameibuka mchezaji bora wa Septemba katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kujinyakulia zawadi ya shilingi milioni moja kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo. Mechi za raundi tano zilizochezwa mwezi Septemba tangu kuanza kwa ligi hiyo ndiyo zimehusishwa kwenye mchakato wa kumpata mshindi wa kwanza. Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto, alisema Kiiza ameisaidia Simba kufanya vizuri ndani ya mwezi huo ikiwemo kufunga ‘hat-trick’ katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar uliochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kiiza aliyefunga mabao matano hadi sasa ameibuka mshindi na kuwapiga bao wachezaji wengine waliokuwa kwenye kinyang’anyiro hicho, Amissi Tambwe wa Yanga na Elius Maguli wa Stand United. Nyota ya mshambuliaji huyo aliyetua Simba akitokea kwa mahasimu wao Yanga, imezidi kung’ara baada ya mwezi uliopita kuchaguliwa na klabu yake kuwa mchezaji wa mwezi. Kiiza ni miongoni mwa wachezaji wanaowania kiatu cha dhahabu Ligi Kuu akiwa amefunga mabao matano sawa na Donald Ngoma wa Yanga huku Maguli akiongoza kwa kufunga sita wakifuatiwa na Tambwe na Kipre Tchetche waliopachika nyavuni mabao manne kila mmoja. Wakati huo huo, TFF imezisogeza mbele mechi za Ligi Kuu ambazo zilipangwa kuchezwa katika raundi ya 11 Novemba 7 na 8, mwaka huu hadi Desemba 12 na 13, mwaka huu ili kupisha maandalizi ya timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ dhidi ya Algeria. Stars inatarajiwa kukutana na Algeria Novemba 14, mwaka huu katika mchezo wa raundi ya pili ya michuano ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi utakaochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kizuguto alisema Stars itaingia kambini mapema mwezi ujao ili kujiandaa na mchezo huo wa awali kabla ya kurudiana ugenini Novemba 17, mwaka huu. Alisema mechi tatu za raundi ya sita ambazo hazikuchezwa Oktoba 4, mwaka huu ili kupisha mechi ya Stars dhidi ya Malawi zimepangwa kufanyika Desemba 16, mwaka huu. Mechi zilizoahirishwa zinaihusisha Yanga dhidi ya African Sports katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Azam FC ikiikaribisha Mtibwa Sugar Uwanja wa Azam Complex huku Simba ikisubiri kupangiwa tarehe ya kucheza na Ndanda FC kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara. | 4 |
Magufuli aliyasema hayo jana kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wakampeni za urais, wabunge na madiwani.Akizungumza mbele ya maelfu ya wana CCM, alisema kuwa hatawatumia wasanii katika siasa tu ila atahakikisha wanafaidika katika maendeleo yao.Alisema kuwa wasanii wamekuwa wakitumiwa katika siasa tu, lakini yeye atakapokuwa rais atahakikisha wasanii hao wanapata maendeleo kama wanavyofaidika wasanii na wachezaji wa Marekani.“Wasanii na wachezaji wa Marekani ni matajiri wakubwa, kwa nini wasanii wetu nao wasifaidike?” alihoji Magufuli katika mkutano huo mkubwa kwa kuhudhuriwa na watu wengi. Aidha, awali mkutano huo ulipambwa na wasanii kibao ambao walitumbuiza na kushangiliwa na umati huo wa watu.Baadhi ya wasanii waliotumbuiza ni pamoja na Dokii, Bushoke, Msechu, Yamoto Band na Thabit Abdul ‘Diamond’, ambaye alipiga vibao viwili tofauti na wenzake walioimba kibao kimoja.Pia Magufuli alisema kuwa wasanii mbali na kutumbuiza pia wana jukumu la kujenga uchumi.Alisema kuwa ataweka mazingira mazuri ili kuwawezesha kupata maendeleo ikiwemo kuanzisha mfuko wa wasanii na wa wachezaji.Naye katibu Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema awali kuwa katika mkutano huo kuna kundi kubwa la wasanii, ambao watatumbuiza katika mkutano huo. Pia alisema yeye ni mpiga tumba mzuri na kipa mzuri, hivyo hatawaangusha wasanii na wachezaji. | 4 |
JUKWAA la Utu wa Mtoto (CDF), limedhamiria kuimarisha na kuwezesha utetezi wa haki za binadamu kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na walioathirika na ndoa za utotoni, ukeketaji na ukatili wa kijinsia.Aidha limedhamiria kuanzisha mazingira rafiki yatakayosaidia na kuimarisha ulinzi na ushiriki endelevu wa watoto katika mipango ya maendeleo. Ofisa Mawasiliano, Utetezi na Mahusiano wa CDF, Michael Jackson aliyasema hayo jijini Dar es Salaam katika mafunzo ya kuwajengea uelewa zaidi wanahabari juu ya ukatili wa kijinsia na namna ya kuripoti matukio ya ukatili nchini yaliyoandaliwa na jukwaa hilo.Alisema katika kuhakikisha jitihada hizo zinafanikiwa, tayari CDF wameanzisha klabu 156 za ndani ya shule na 55 za nje ya shule ambapo pia wameunda kamati za ulinzi wa mtoto tatu kiwilaya na moja ya kikanda. Aidha alisema wasichana 903 waliopo ndani na nje ya shule walipewa elimu juu ya afya ya uzazi na ujuzi wa maisha na wasichana 153 wanajishughulisha na kazi za kujiongezea kipato.“Katika kipindi cha mwaka 2016-2018 tumeweza kuwapatia wasichana 522 mafunzo ya ujuzi wa biashara na ujasiriamali, sambamba na kufanya vipindi vinavyohusu haki za watoto, ukeketaji, ujasiriamali, mimba za utotoni na ndoa za utotoni,”alisema | 3 |
KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu, Mzee Mkongea Ali ameutaka uongozi wa Wilaya ya Mpwapwa kuhakikisha maji yanapatikana saa 24.Alitoa maagizo hayo wakati wa kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Wodi ya Utapiamlo Mkali katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa baada ya kuridhishwa na ujenzi wake.Wodi hiyo inajengwa kutokana na utafiti uliofanywa mwaka 2017/2018 kuonesha kuwa kati ya watoto 70,117 waliopimwa asilimia 37 kati yao wana udumavu, asilimia 12 wana uzito pungufu na asilimia moja wana unyafuzi.Ali alisema ameridhishwa na ujenzi na kutaka uongozi wa wilaya hiyo kuhakikisha maji yanakuwepo saa 24.“Watu wanaweza wakajiuliza kwa nini tunatumia muda mrefu kukagua wakati fedha ni za wafadhili, lakini ikumbukwe kuwa hawa ndugu zetu wametoa kodi za wananchi wao ili kusaidia nchi yetu, hivyo ni lazima tuwe na uchungu ili kuwapa shauku ya kuendelea kutusaidia,”alisema.Akizungumza baada ya maelekezo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri alisema aliahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote waliyopewa.“Maelekezo uliyoyatoa tumeyapokea na tutayatekeleza na kuhusu maji tayari tulishaanza kufanyia kazi na tutajitahidi kuhakikisha huduma hii inapatikana kwa saa 24,”alisema.Naye Mganga Mkuu wa Wilaya, Dk Arcard Rwezaula alisema lengo la kujengwa wodi hiyo ni kutoa matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali chini ya miaka mitano.“Mwaka 2017/2018 wakati wa utoaji wa matone ya vitamini A, minyoo na upimaji wa hali ya lishe chini ya miaka tano ulionesha uwepo wa tatizo la utapiamlo mkali, hivyo jambo ambalo kwa kushirikiana na wadau tukaona tujenge wodi ya kutolea matibabu ya utapiamlo mkali katika wilaya yetu,”alisema.Akifafanua hatua ambazo zimechukuliwa mpaka sasa, Dk Rwezaula alisema vituo vyote 62 vya kutolea huduma katika halmashauri hiyo wahudumu wake wamefundishwa namna ya kuwatambua na kuwapatia huduma watoto wenye utapiamlo.Miradi mingine iliyotembelewa kuzinduliwa ni mradi wa miundombinu ya mnada wa wanyama, ufugaji nyuki wa Kwamshango ambapo mizinga 28 iligawiwa kwa vikundi vya ufugaji na kuzindua maktaba ya Shule ya Sekondari ya Kibakwe. | 3 |
.Rais John Magufuli kwa nyakati tofauti amekutana na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Dkt Stergomena Tax na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Manfred Fanti Ikulu jijini Dar es salaam.Baada ya mazungumzo yake na Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa SADC, Dkt Stergomena Tax amesema kuwa alikuja kutoa taarifa ya utekelezaji wa masuala mbalimbali ya Jumuiya hiyo ikiwemo uendelezaji wa viwanda na kanda huru ya biashara ambapo wamekubaliana kuendelea kuhamasisha nchi Wanachama kuendeleza viwanda ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi.Ameelezea baadhi ya maeneo yaliyopo katika mkakati wa kukuza uchumi wa SADC kuwa ni kuendeleza miundombinu hasa ya usafiri na nishati ambayo bado ni changamoto kwa nchi za SADC, na pia ameipongeza Tanzania kwa hatua inazoendelea kuchukuliwa ikiwemo ujenzi wa barabara, reli na kuongeza uzalishaji wa umeme.Kwa upande wake Balozi wa EU nchini Manfred Fanti amesema kuwa, mazungumzo yake na Rais Magufuli yamekuwa na manufaa makubwa ambapo wamejadili maendeleo mazuri ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na EU, na kwamba katika siku za karibuni wamekamilisha mazungumzo yaliyoruhusu kuendelea kwa mpango wa Jumuiya hiyo kuchangia bajeti ya maendeleo ya Tanzania ambapo shilingi Bilioni 132 zilizokuwa zimezuiwa zimeruhusiwa na sasa wanaandaa mpango mwingine wa miaka Saba utakaoanza mwaka huu.Balozi Fanti amesema kuwa, kwa jinsi anavyoyaona maendeleo ya Tanzania ana matumaini makubwa kuwa EU itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na Tanzania.Rais Magufuli amemshukuru Balozi Fanti kwa juhudi zake za kuimarisha uhusiano wa Tanzania na EU na amemhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na EU katika masuala mbalimbali yenye maslahi kwa pande zote mbili. | 3 |
Kulwa Mzee – Dar Salaam MKURUGENZI
wa Mashtaka nchini (DPP), Biswalo Mganga, amesema taarifa alizotoa Mbunge wa
Arusha mjini, Godbless Lema, kuhusu kuuawa kwa watu 13 ni za upotoshaji na
hivyo watamchukulia hatua. Alisema hivi
karibuni Lema alikamatwa mkoani Singida kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo kwamba
watu hao wameuawa bila Serikali kuchukua hatua. Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Biswalo alisema; “sitajali mwanasiasa wa
chama chochote, rangi, kabila au cheo, yeyoto anayefanya makosa atafunguliwa
mashtaka, na kwa hili nitachukua hatua, hawawezi kuendelea na upotoshaji wa
aina hiyo. “Watanzania
wana haki ya kutoa maoni, lakini wasitumie haki hiyo kwa masilahi yao binafsi,
iwe wanasiasa au raia, kama mtu anadiriki kusema kuna watu 13 wameuliwa na
mmoja kuchomwa moto, ana lengo la kuitishia amani. “Katiba
ya nchi inakupatia uhuru wa kujieleza, lakini hakuna uhuru usio na mipaka,
tusikimbilie haki za binadamu. “Hatuwezi
kutumia kigezo cha haki za binadamu kuvunja umoja na amani ya nchi kwa sababu
una haki ya kusema chochote,” alisema Biswalo. Alisema Lema
ameorodhesha kesi nane na kudai Jumanne Nderema alichinjwa na Serikali
haijafanya lolote, tukio la Feb 5, mwaka huu eneo la Sasajila, Manyoni DPP akifafanua
matukio ya vifo aliyoyataja Lema, alisema Hamis Chadem (25) amekamatwa na
sababu ya kifo cha Jumanne ni mwili kukutwa na majeraha na sehemu ya shingo
imekatwa. Alisema marehemu
na mshtakiwa ni mtu na kaka yake, ambapo alikuwa akimtuhumu kufanya mapenzi na
shemeji yake, hivyo alimvizia alipolala na kumkata na kesi namba 4 ya mwaka huu
imefunguliwa Mahakama ya Wilaya ya Manyoni. Pia alimtaja
Issa Abdallah tukio lililotokea Januari 23 eneo la Sanjalanda, ambapo polisi
wamefungua jalada kwa mshtakiwa Maria Robert (21). Alisema marehemu
hakuchinjwa na taarifa ya daktari inaonyesha ni mtoto wa kuzaliwa na mshtakiwa
huyo, alikuwa na mgogoro na mumewe ambaye alikuwa hampatii matunzo hivyo
alimnyonga mtoto wake mpaka kufa na akatoa taarifa za uongo Januari 27, amefunguliwa
kesi ya mauaji namba 3 ya mwaka huu. “Tukio
la Novemba 21 mwaka jana, Mnyambelele Nyandu wa Itigi anadai amechinjwa,
anarukia mambo ambayo hayawahusu, Myambelele Nyandu ni mshtakiwa kamuua mkewe
Shoma Ngasa. Mshtakiwa ana wake wawili, mwengine ni Ana Makilrma, aliwapiga
viboko wake zake na wakiwa ndani alimpiga mpaka kusababisha kifo chake,
alifunguliwa kesi namba 22/2019. “Tukio
la Martin Motelewa, alichomwa moto. Washtakiwa Msem Hamidu (33) na Athanas
Stephani maarufu Manyama walikamatwa, taarifa ya daktari na maelezo kwenye
jalada ni kupigwa na kitu kizito usoni na kuchomwa moto, alikuwa amelala kwenye
pagale, hakuna ushahidi wa kuwaunganisha watuhumiwa, hivyo walihojiwa na
kuachiwa. “Alex
Jonas wa Manyoni mjini ni Katibu Mwenezi Wilaya Manyoni (Chadema), tukio la Februari
26 mwaka huu na sababu ya kifo ni kuvuja damu nyingi, alikuwa na majeraha
upande wa uso na hadi sasa hakuna mshtakiwa aliyekamatwa na polisi wanaendelea
na upelelezi. Aliuawa, lakini hakuchinjwa, alikatwa kwenye paji la uso,” alisema
Biswalo. Alisema Lema
alidai pia Msechelela Leonard alichinjwa, lakini polisi wamefungua jalada na
washtakiwa ni Rashidi Rashidi (34), Timothy Kindulu na Gervas maarufu Etoo. Biswalo alisema
marehemu alikuwa ni mtoto wa diwani wa CCM, alivuja damu kutokana na majeraha
kichwani na michubuko tumboni, lakini hakuna maelezo kama alichinjwa. “Kwanini
watoe taarifa za uongo, kwamba Serikali na watu wake hawafanyi kitu chochote,
tufanye siasa zenye ustaarabu, hakuna haki pasipo wajibu, kifungu 9 cha makosa
ya jinai nawajibika kwenda kutoa taarifa polisi kueleza. “Aje (Lema)
aniambie ni lini alienda kutoa taarifa na kwamba hao watu anawafahamu, hatuwezi
kuendelea kuwa na watu kueneza taarifa za uzushi na zenye kueneza chuki na
kusababisha watu wakae kwa mihemuko kwamba hakuna amani. “Baadhi
ya watu wanasema wanachama wa upinzani wanaonewa wakati wanafanya mambo ya
kipuuzi, usijifiche kwenye siasa, iwe CCM au chama chochote kwa kufanya watu
waishi kwa hofu, haki za kikatiba zisije zikaathiri mambo ya watu wengine,”
alisema Biswalo. | 3 |
TIMU ya Azam FC jana iliibuka na ushindi na kunyakua pointi tatu baada ya kuifunga Polisi Tanzania bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Ushirika Moshi.Ushindi wa Azam ulipatikana dakika ya nane kupitia bao pekee lilopachikwa kimiani na Obrey Chirwa kwa kichwa akimalizia pasi iliyochongwa na Bruce Kangwa. Matokeo hayo yamewafanya Azam kufikisha pointi 23 na kupanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo, huku wapinzani wao wakisalia nafasi ya tisa kwa pointi 19.Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa kila upande, lakini Azam walionekana bora zaidi kwa kutengeneza mashambulizi ya hatari zaidi kwa kupiga pasi ndefu. Baada ya bao hilo wenyeji Polisi Tanzania walionekana kuchangamka kwa kucheza mpira wa nguvu uliowafanya wachezaji wa Azam kuanguka mara kwa mara na kutumia udhaifu huo kutengeneza mashambulizi mawili dakika ya 20 na 29 ambayo hayakuwapa faida hadi timu hizo zilipoenda mapumziko.Wakati vikosi vinaingia kipindi cha pili, mchezo ulilazimika kusimamishwa kwa muda kupisha kukolezwa chokaa kwa alama za uwanja huo baada ya kufutika na baadae mchezo uliendelea kwa kasi huku Azam wakicheza mpira wa malengo kwa kurudi nyuma kulinda ushindi waliovuna kipindi cha kwanza na kuwaacha wenyeji wakitawala sehemu ya kiungo kwa kuchezea mpira.Dakika ya 75 mchezaji wa Polisi Tanzania Baraka Majogoro nusura afunge bao la kusawazisha akitumia vema mpira wa adhabu ndogo na kuachia shuti kali lilotambaa chini na kupangulia na kipa Razak Abarola.Shambulizi hilo lilionekana kuendelea kuwapa nguvu Polisi walionekana kuzidisha mashambulizi ambayo wachezaji wa Azam waliyazima kutokana na muda mwingi walikuwa wanacheza kwa kujilinda zaidi hali iliyowafanya mchezo huo kukamilika kwa Azam kuibuka na ushindi. Matokeo mengine ya mechi za ligi hiyo zilizochezwa jana, JKT Tanzania ilikubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Namungo FC katika mchezo uliochezwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.Kwenye mchezo huo ushindi wa Namungo ulipatikana kupitia bao pekee lilopachikwa kimiani na mchezaji Bigrimana Blaisé dakika ya 90 na kutosha kabisa kuwanufaisha kwa kujizolea pointi tatu. Kwa matokeo hayo Namungo imepanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo ikifikisha pointi 22 na wapinzani wao wakisalia nafasi ya 10 wakiwa na pointi 19. | 4 |
Na Mwandishi wetu, Kigoma WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kazi na mifumo ya ukusanyaji wa takwimu ili kuwa na takwimu bora kwa ajili ya kutunga sera na kupanga mipango endelevu ya maendeleo ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuifanyia tathmini na ufuatiliaji mipango hiyo. Dk. Mpango aliyasema hayo wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la Ofisi ya Taifa ya Takwimu mkoani Kigoma. “Jengo hili litakapokamilika litaboresha utendaji kazi kwa watumishi na upatikanaji na usambazaji wa takwimu kwa wadau wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu na hususani wakati huu wa maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika mwaka 2022” alisema Dk. Mpango Aliipongeza Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa namna ambavyo imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa weledi na kuipatia nchi takwimu bora ambazo ndizo zinatumika katika kusukuma gurudumu la maendeleo. “Mafanikio ya Serikali yetu ya awamu ya tano ambayo tunajivunia yamejengwa kwa msingi mzuri wa matumizi bora ya takwimu ambazo zinazalishwa na taasisi yetu hii,”alisema Dk Mpango. Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dk. Albina Chuwa, alisema ujenzi wa jengo hilo ni miongoni mwa mikakati ya ofisi yake ya kuboresha miundombinu itakayo wezesha matumizi ya teknoljia ya kisasa katika shughuli za ukusanyaji na uchakataji wa takwimu mbalimbali hatua iliyolenga kupunguza matumizi ya Serikali. Ujenzi wa jengo hilo ulioanza mwaka 1994 chini ya ufadhili wa Ofisi ya Takwimu ya Sweden (Statistics Sweden) iliyokuwa na ushirikiano na Idara Kuu ya Takwimu chini ya Wizara ya Mipango. Statistics Sweden kwa mujibu wa kumbukumbu zilizoko waligharamia jengo hili kwa jumla ya Shillingi milioni tano mwaka 1994 na Serikali za Awamu ya Tatu, na Nne ziliendelea na juhudi za kugharamia ujenzi wake hadi lilipofikia kwa gharama ya shilingi 173,386,000. | 3 |
KAMPALA, Uganda MBUNGE wa Jimbo la
Kyadondo Mashariki, Robert
Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine,
amekamatwa tena baada ya mashabiki wake
kupambana na polisi wakipinga kufutwa matamasha yake ya Pasaka yaliyokuwa yafanyike mjini hapa
na katika miji ya Arua na Lira. Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor, hali ya
taharuki ilianza baada ya polisi kuzuia msafara uliokuwa ukiongozwa na mbunge
huyo kwenda katika ufukwe wa One Love uliopo eneo la Busabala. Taarifa za gazeti hilo zilieleza kuwa baada ya Bobi
Wine kukamatwa alitumbukizwa ndani ya gari la polisi na kupelekwa mahali kusikojulikana . Mashuhuda wa tukio hilo walieleza kuwa kabla ya ya
mbunge huyo kukamatwa polisi wa kutuliza ghasia walivunja kioo cha gari
lake na kumvuta nje, lakini mwimbaji
Nubian Li ambaye alikuwa naye hakukamatwa. Mbali na mbunge huyo, waandaaji mashuhuri wa
matamasha ya muziki Andrew Mukasa na Abbey Musinguzi maarufu kama Abtex ambao waliandaa tamasha hilo la Bobi Wine nao walikamatwa jana. Taarifa zinaeleza kuwa wawili hao walikamatwa mapema
jana na kuzuiliwa katika gari moja la maofisa
wa polisi kabla gari hilo kuondoka nao. Kukamatwa kwa mbunge huyo ni baada ya Rais Yoweri
Museveni kusema kuwa hatakubali matamasha ya muziki uliojaa siasa na kuonya
kwamba katika siku zijazo hakuna mtu atakayefidiwa kwa matamasha ambayo
yamefutiliwa mbali kutokana na siasa. Rais huyo alitoa onyo hilo wakati wa mkutano na
wanachama na waandaaji matamasha ya muziki nchini hapa na wamiliki wa maeneo ya
kumbi za muziki katika Ikulu ambako alitoa Sh bilioni mbili za Uganda kama
fidia ya hasara waliyopata baada ya maofisa wa polisi kufutilia mbali matamasha
ya muziki wa Bobi Wine. | 2 |
NA ZAINAB IDDY KOCHA Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, amesema licha ya kutofanya usajili katika kikosi chake hadi sasa katika usajili wa dirisha dogo, mwendo wao utakuwa ni ule ule kama walioanza nao Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu. Katika msimamo wa ligi hiyo hadi sasa Mtibwa Sugar imecheza mechi tisa ambapo imeshinda mechi saba, sare moja na kupoteza mmoja. Kwa matokeo hayo, Mtibwa inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 22 nyuma ya Yanga waliopo nafasi ya pili kwa pointi 23 na Azam wanaoongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 25. Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi, Mexime ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, alisema licha ya kutokuwepo na mabadiliko makubwa katika kikosi chake bado kitaendelea kutembeza dozi kwa kila timu watakayokutana nayo. “Tulivyoanza ndivyo tutakavyomaliza kwani lengo letu ni kuona msimu huu Mtibwa inamaliza katika nafasi tatu za juu baada ya kushindwa kuyafikia malengo hayo kwenye kipindi kirefu kilichopita. Mtibwa Sugar leo itakuwa ugenini katika Uwanja wa Sokoine, Mbeya kuwakabili wenyeji wao, Mbeya City. | 4 |
SERIKALI imeeleza Bunge mikakati ya kuboresha vyombo vyake vya habari, ikiwamo kuongeza mapato ya Kampuni ya Serikali ya Magazeti (TSN) na kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) lifanye kazi kwa umakini.Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shoza wakati akijibu hoja mbali mbali za wabunge kabla ya kupitishwa makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2019/20.Kampuni ya TSN ambayo inachapisha magazeti ya Daily News, Sunday News, Habari- Leo na SpotiLeo, jukumu lake kubwa ni kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha wananchi kwa njia ya magazeti. Shonza alikiri TSN kulikuwa na changamoto ya muda mrefu ya upungufu wa mapato kutokana na mapato kushuka, kulikochangiwa na ushindani unaotokana na maendeleo ya teknolojia katika sekta ya uchapaji.“Sisi kama wizara tumeliona,” alisema na kufafanua kuwa kwa kushirikiana na TSN, serikali imekuja na mpango wa kutumia changamoto hiyo kama fursa kwa kuanzisha Televisheni Mtandao (Daily News Digital). Alisema televisheni hiyo, inafanya kazi vizuri na ndani ya muda mfupi, yameonekana mafanikio makubwa kutokana na watazamaji kuongezeka na imeongeza mapato.Katika hotuba yake bungeni, Dk Harrison Mwakyembe alisema hadi Machi mwaka huu, idadi ya wafuatiliaji kwenye televisheni mtandao hiyo ilifikia watu 47,000. Akizungumzia maslahi duni ya wafanyakazi wa TBC, Naibu Waziri alisema hatua mbali mbali zimechukuliwa ikiwamo kupeleka ombi kwa Msajili wa Hazina, aboreshe mishahara katika mwaka ujao wa fedha.Maslahi yataboreshwa ikiwa ni pamoja na kulipa malimbikizo yote yanayodaiwa. Kuhusu tatizo la uchakavu wa mitambo, alisema bajeti ya uboreshaji imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka na katika mwaka ujao wa fedha shirika limetengewa Sh bilioni tano. Alisema serikali ina nia ya dhati kuhakikisha inaboresha na kuhakikisha shirika linafanya kazi yake kwa umakini.TBC lilianzishwa kwa Tangazo la Serikali Namba 186 la 2007 chini ya Sheria ya Mashirika ya Umma ya mwaka 1992. Shirika linamiliki vituo vitatu vya televisheni vya TBC 1, TBC 2 na TBC 3 (Tanzania Safari Channel) na kwa upande wa redio, linamiliki idhaa tatu za TBC Taifa, TBC FM na TBC International. Akijibu hoja kuhusu matangazo mubashara yanayoonesha ziara za Rais, Shonza alisema serikali haiwezi kuacha kuonesha ziara hizo kwa sababu kinachooneshwa ni maendeleo kwa ajili ya wananchi. | 3 |
MKUU wa mkoa wa Lindi, Geoffrey Zambi amewataka wadau wa misitu kuhakikisha kwamba misitu hiyo haivunwi kiholela kama vile watu wote watakufa kesho. Aidha aliwataka viongozi na wafanyabiashara kuwa waadilifu na waaminifu katika uvunaji wa mazao ya misitu ili kuleta uendelevu unaotakiwa.Mkuu huyo wa Mkoa alitoa kauli hizo wakati akizindua warsha ya siku moja ya wadau wa biashara ya mazao ya misitu iliyofanyika wilayani Kilwa na kushirikisha mikoa mitatu ya Lindi, Pwani na Ruvuma. Warsha hiyo iliyoendeshwa na Shirika la Mpingo na Maendeleo (MCDI) na kufadhiliwa na Shirika la Uhifadhi Duniani (WWF) ilikuwa na mada tatu zilizojadili uendeshaji wa biashara, masoko na uendelezaji wa misitu.Alisema kwamba viongozi wengi katika vijiji wamekuwa uaminifu na kusababisha uvunaji haramu wa misitu unaoleta hasara kubwa kwa vijiji vyenyewe na taifa. Zambi alisema amekuwa akikutana na watu wanaovuna misitu bila kibali, wengine vikiwa vimeisha lakini ukihoji unagundua kwamba wapo viongozi wa vijiji na wanaona hali hiyo lakini kwa kukosa uaminifu na uzalendo wanaacha hali hiyo ikiendelea. Alitaka viongozi hao kukoma tabia ya ulaji rushwa na kutojitambua na kushirikiana na wadau wengine kama wakala wa misitu na uongozi wa misitu ya vijiji ili kuiwezesha kuwa na uvunaji endelevu wenye tija. Pia katika warsha hiyo aliwataka wafanyabiashara kuangalia sheria na taratibu na kuonesha penye kasoro lakini akahimiza wao kuwa waadilifu katika biashara hiyo ikiwamo upataji wa vibali,ulipaji kodi na ushuru mwingine ili kuwa na uhakika wa faida kurejea kwa wananchi wanaolinda misitu hiyo.“Msifanye mambo kwa kukwepa kodi ili kufanikisha biashara zenu,” alisema Zambi na kuwahimiza kufuata utaratibu za uvunaji ili kuwa na uhakika wa mazao hayo kutumikia wananchi leo na kesho. Aliisifu MCDI kwa kuweka warsha hiyo iliyoshirikisha maofisa wa serikali, kutoka idara mbalimbali ikiwamo Mamlaka ya Kodi, wafanyabiashara na wenye viwanda ili kuweza kusaidia katika kuhakikisha kwamba kuna kuwa na uvunaji endelevu wenye kuleta tija kwa wananchi .“MCDI imesaidia kubadilisha maisha ya watu wetu toka mlipoanza mwaka 2007, endeleeni kuhakikisha kwamba misitu inaendelea kuwapo huku ikiwatumikia wananchi,” alisema Zambi. Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kuhutubia, Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Christopher Ngubiagai alisema kwa kuwa katika biashara kuna mambo mbalimbali ya msingi, aliwataka wafanyabiashara na wadau wengine kuimarisha mabaraza ya majadiliano ili kuboresha uhusiano wa sekta binafsi na serikali. Aliutaka pia mkutano huo kuja na azimio litakaloboresha uwazi ili kuwepo na hali ya kuaminiana na kuweka sawa mazingira ya biashara. “Haitoshi kulalamika, bali kujadiliana na kuona njia nzuri ya kufanikisha kazi zetu,” alisema.Mtendaji wa MCDI, Jasper Makala alisema warsha hiyo ni mfululizo wa warsha zilizofanyika kwa siku tatu kuhusu hifadhi ya misitu na kuifanya endelevu na kuvipatia vijiji vinavyozunguka, tija. Aidha alisema warsha hizo zililenga kupambanua changamoto mbalimbali na kutoka maazimio ya namna ya kuenenda katika kufanikisha uvunaji endelevu wa misitu bila kudhuru mazingira. Na Frank Leonard, Iringa SHILINGI milioni 430 zimeingizwa katika mzunguko wa fedha wa mjini Iringa kupitia mikopo ya Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo (SIFA Saccos Ltd) kati ya Januari na Septemba mwaka huu. Mwenyekiti wa Saccos hiyo, Emmanuel Magoda alisema kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika mjini Iringa hivi karibuni kwamba mikopo hiyo imetolewa ili kusaidia ukuaji uchumi.Alisema kati yake, Sh milioni 223 zimetolewa kwa ajili ya mikopo ya biashara, Sh milioni 184 mikopo ya walaji na zaidi ya Sh milioni 17 kama mikopo ya dharula, Sh milioni saba mikopo ya mshahara na Sh 500,000 kwa ajili ya mkopo wa kilimo kuchangia Pato la Taifa na kuchochea ajira katika sekta binafsi.“Tuna imani wajasiriamali waliopata fedha hizo hawakuzichimbia ardhini bali waliziingiza kwenye mzunguko wa fedha katika mji wetu wa Iringa hatua itakayosaidia kuchochea maendeleo,” alisema. Akizungumzia mafanikio ya Saccos hiyo yenye wanachama zaidi ya 900, Magoda alisema mpaka Septemba mwaka huu walikuwa na hisa zenye thamani ya Sh milioni 131.6 akiba yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 156.9 na amana ya zaidi ya Sh milioni 67.3 na akiba maalumu ya Sh milioni saba. Alisema SIFA Saccos Ltd imeendelea kuendeshwa kwa faida licha ya hali ya uchumi kubadilika badilika hatua iliyowawezesha wanachama wake kufaidika kwa kupata faida juu ya akiba na amana zao.“Maendeleo ya biashara ya fedha ilianza kwa kusuasua mwanzoni mwa mwaka huu wa fedha, hata hivyo imeendelea kuimarika kwa kadri miezi inavyosogea,” alisema. Alitaja mafanikio waliyopata kuwa ni pamoja na kupokea maombi ya wanachama wapya 105 na kumaliza kulipa mkopo waliokopa kutoka Mradi wa Kutoa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo (SELF). Alisema chama kinakisia kutoa mikopo yenye thamani ya Sh Milioni 740 mwakani sambamba na elimu kwa wanachama juu ya dhana ya ushirika, haki na wajibu wao na elimu juu ya masuala ya fedha. “Matarajio yetu wanachama wengi zaidi wataomba mikopo mwakani baada ya dalili za kuimarika kwa uchumi kuanza kuonekana,” alisema.Aliwataka wanachama wa Saccos hiyo kutumia huduma za chama hicho hatua itakayokijenga zaidi kwa maendeleo yao na ya taifa. Na Mwandishi Wetu WANANCHI wa mkoa wa Mtwara wamehimizwa kujitokeza katika banda la Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kupatiwa elimu ya ujasiriamali na kujiandikisha kwenye maonesho ya viwanda vidogo ambayo yalianza hivi karibuni na yanatarajiwa kumalizika Novemba 11, mwaka huu mjini Mtwara. Akizungumzia ushiriki wao, Meneja wa NSSF mkoani humo, Stanley Milanzi alisema wanataka kutumia fursa hiyo kuwaelimisha wananchi huduma zao ili waamue kujiunga kwa manufaa ya maisha ya baadaye.“Tukikaa ofisini wananchi hawawezi kutambua kile tunachokifanya, ndio maana tunatumia fursa ya kushiriki maonesho mbalimbali kutoa elimu ya kujiandikisha na kujiunga na huduma zetu, tunawahimiza wajitokeze kwa wingi na watafurahia manufaa,”alisema na kutaka wananchi wengi zaidi kujiandikisha. Milanzi alisema anaamini kuna wajasiriamali wengi watakaojiunga na mfuko wao hawatajuta, kwani watanufaika na mafao yatolewayo na shirika hilo na kupata bima ya matibabu bure kwao na familia zao.Alisema wajasiriamali watakaojiunga nao kuwa wanachama wanaweza kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa kwao ikiwemo mikopo ya kujiendeleza kiuchumi.“Kuna fursa nyingi kwetu hasa kama watu watajiunga kwa vikundi vya wakulima, wafanyabiashara au kundi la madereva waliosajiliwa,”alisema. Alisema shirika hilo limekuwa likiingia makubaliano na taasisi mbalimbali za kifedha ili mradi kuwasaidia wanachama wake walio hai kunufaika na huduma za kimaendeleo na kiuchumi.Milanzi alisema hii sio mara ya kwanza kwao kushiriki maonesho ya aina hiyo kwani wamekuwa wakishiriki kila mkoa ili kuelimisha jamii kuhusu huduma zao na umuhimu wa watu kujiandikisha. Alisema lengo la maonesho hayo ni kuwasaidia wajasiriamali kupata masoko ya bidhaa zao, kujifunza kupitia wenzao na kujenga mahusiano baina ya taasisi moja na nyingine. Alisema maonyesho hayo yameshirikisha taasisi 16 za kiserikali na wajasiriamali zaidi ya 250 kutoka Mtwara na mikoa jirani. Mkuu wa mkoa | 3 |
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge, ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutoa taarifa ya hatua iliyofi kiwa ya wawekezaji wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) kilichoonesha nia ya kuwekeza jijini hapa.Dk Mahenge ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) alitoa agizo hilo baada ya kamati hiyo kupokea taarifa ya utekelezaji wa uhamasishaji na kuwezesha uwekezaji mkoani humo juzi.Akiwasilisha taarifa hiyo, Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Dodoma anayesimamia sekta ya uchumi na uzalishaji, Aziza Mumba, alisema TBL pamoja na kuonesha nia ya kuwekeza, lakini uongozi wa halmashauri ya jiji hilo haujashughulikia suala hilo.Taarifa iliyowasilishwa kwenye kikao cha kamati hiyo zinaonesha kuwa, mpaka sasa TBL haijapewa ardhi, japokuwa maandalizi ya uwekezaji huo yameanza. Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy, alisema bado kuna changamoto katika utoaji wa ardhi kwa wawekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kushauri kutengwa ardhi ya uwekezaji na kuwekwa sharti la kumtaka mwekezaji kutoa sehemu ya gharama ambayo haitarudishwa.“Mfano TBL imeonesha nia ya kutaka kujenga kiwanda chenye uwezo mkubwa kwa Afrika Mashariki na Kati na waliomba kupewa ardhi lakini mpaka sasa hawajapewa. Tumepeleka wawekezaji wengi jiji lakini hakuna wanaowashughulikia, ni lazima kuwe na utaratibu unaoonesha wawekezaji wangapi wamefika hapo, wangapi wako tayari kuwekeza na wangapi wamehudumiwa,” alisema.Kutokana na maelezo hayo, Dk Mahenge aliutaka uongozi wa jiji la Dodoma kutoa taarifa ya kina ya hatua iliyofikiwa. “Inasikitisha kuona wawekezaji kama TBL ambao wanataka kujenga kiwanda cha kuzalisha pombe zaidi ya lita milioni sita ikiwa ni maradufu ya uzalishaji wa kiwanda cha Dar es Salaam bado mpaka sasa hawajashughulikiwa.”“Na hawa waliomba ardhi ya kujenga kiwanda, hili lishughulikiwe kwa haraka tunavyochelewa chelewa unaweza kuja sikia wameenda kuwekeza nchi nyingine,” alisema.Kuhusu kiwanda cha sukari kilichokuwa kijengwe katika Halmashauri ya Chamwino, Mumba alisema mwekezaji wa kiwanda cha Parandera Industries Ltd pamoja na kupewa ardhi katika kijiji cha Dabalo, ameshindwa kukamilisha uwekezaji kutokana kukosa barabara ya kupitisha mitambo kiwanda hicho. Kutokana na maelezo hayo, Dk Mahenge alitaka kupitiwa upya kwa mkataba wa mwekezaji huyo ili asije kutumia fursa ya kupewa ardhi kufanya shughuli nyingize nje ya makubaliano ya uwezezaji.“Huyu mwekezaji mimi mwenyewe nilikuwa miongoni mwa waliosimamia apewe ardhi kwa ajili ya uwekezaji na hata Waziri Lukuvi (William, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi) alilisimamia hili vizuri, sasa iweje leo anasema hakuna barabara ya kupitisha mitambo, hakikisheni mkataba wake unaangaliwa isije mtu akawa amepewa ardhi ameitumia tofauti na makubaliano ya uwekezaji,” alisema.Awali, Mumba alieleza changamoto kadhaa zinazokwaza kasi ya uwekezaji mkoani Dodoma ikiwamo maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji kutopimwa na yaliyochukuliwa kutolipwa fidia, kukosekana kwa miundombinu kama maji, umeme na barabara katika maeneo ya uwekezaji na kuchelewa kwa hati na vibali vya ujenzi. | 3 |
KAMPUNI ya Mawasiliano ya Tigo imemkabidhi nyumba ya vyumba 17 ikiwa na samani zote za ndani Babu Joram Mollel (93), kutokana na ushiriki wake wenye mafanikio katika Tigo Kili Half Marathon kwa miaka minne mfululizo.Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika eneo la Mushono nje kidogo ya Jiji la Arusha, ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo, Simon Karikari pamoja na Ofisa Biashara Mkuu, Tarik Boudiaf.Akizungumza kwenye hafla hiyo, Karikari alisema nyumba hiyo ilinunuliwa na kukarabatiwa kisha kumkabidhi Babu Mollel kama ishara ya shukrani kwa kujituma na umahiri wake katika riadha.‘Babu Mollel amekuwa akishiriki mashindano ya Tigo Kili Half Marathon kwa miaka mingi sasa. Tulipoona hali ya makazi yake si nzuri, Tigo tuliona njia sahihi ni kuwezesha apate nyumba yake mwenyewe,” amesema Karikari.“Katika nyumba yake hii ya hapa Mushono, Babu atakuwa anakaa katika nyumba ya kisasa, iliyo tayari na samani pamoja na vyombo vyote muhimu vya ndani. Nyumba hii pia imeunganishwa na umeme na maji. Hati ya nyumba pia ipo kwa jina lake, hivyo yeye ndiye mmiliki halali wa nyumba hii,” aliongeza Karikari.Aidan Komba, ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Kaskazini alisema kwamba nyumba imegawanyika sehemu tatu na kuongeza kuwa Babu Mollel atakaa katika nyumba moja na mbili zilizobaki ataweza kuzipangisha na kujipatia kipato cha kuendeshea maisha yake ya kila siku.“Napenda kuwashukuru sana Tigo kwa zawadi hii ya kipekee. Maneno yangu hayawezi kuelezea furaha niliyonayo. Kitendo hiki kina maana kubwa sana kwangu. Maana hivi sasa ninaweza nikasema sasa nina mahali pakuita kwangu,” alisema Babu Mollel.Ushiriki wa Babu Mollel katika mashindano ya Kili Marathon ni wa zaidi ya miaka 15, ambapo amekuwa akiwavutia watu wengi kumshangilia wakati akishiriki mbio za marathon, pamoja na uzee wake.Katika miaka minne mfululizo iliyopita, Tigo imekuwa mlezi na mdhamini mkuu wa mbio za kilometa 21 zinayojulikana kama ‘Tigo Kili Half-Marathon’, ambayo ni nusu ya mbio kamili ya kilometa 42 za marathon ambayo hufanyika katika vilima vya Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu kuliko yote barani Afrika.Mwaka jana, Tigo ilishirikiana na Babu Mollel katika kampeni maalumu ya Tigo Kili Half-Marathon iliyoitwa ‘Tisha kama Babu’. Kampeni hiyo ilikuwa na lengo kubwa la kuhamasisha Watanzania kuweza kuishi maisha ya kujali afya zao.Wakati huo huo, Tigo mwaka jana ilisitisha rasmi matumizi ya namba ya mbio aliyokuwa akiitumia Babu Mollel ‘1040’ na alitambuliwa rasmi kama mwanamichezo wa heshima ‘Hall of Fame’. | 4 |
MKUU wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme amesema kufungwa kwa Benki ya Wananchi ya Mbinga mkoani humo kumeathiri kiasi kikubwa uchumi wa wakulima na jamii.Mndeme amesema hayo jana kwenye ufunguzi wa Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Maendeleo ya mkoa wa Ruvuma (RCC) mjini Songea.Amesema kufungwa benki hiyo kumesababisha baadhi ya wakulima kutomudu gharama za uendeshaji kilimo kwa kukosa mikopo ya pembejeo za kilimo iliyokuwa ikitolewa nao.Alisema ili kukabiliana na hilo, serikali imeanza kuchukua hatua dhidi ya walioifilisi benki hiyo na kuikabidhi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi.Mkuu wa mkoa alihimiza wataalamu kuzitumia mvua zilizoanza kunyesha mkoani humo kwa ajili ya kwenda kutoa elimu ya kilimo bora kwa wakulima vijijini, badala ya kukaa ofisini tu.Ametoa onyo kwa mawakala ambao watauza pembejeo za kilimo kwa bei kubwa tofauti na bei elekezi ya serikali.Alisema atakayeenda kinyume atachukuliwa hatua kali za kisheria. Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro amesema migogoro kati ya wakulima na wafugaji inazidi kuongezeka hivyo ameshauri kujengwa kwa majosho na kutengwa kwa matumizi bora ya ardhi kubaini mae | 5 |
TANGAWIZI ni kiungo kinachotokana na mizizi ya mmea wa tangawizi. Mmea huu unafanana na binzari ikiwa bado haijamenywa maganda yake. Kwa hapa Tanzania, hulimwa zaidi katika mikoa ya nyanda za juu kusini na baadhi ya mikoa kama Kilimanjaro, baadhi ya maeneo ya mkoa wa Manyara, Morogoro na kwingineko. Pia kama bidhaa inapatikana nchi nzima kwa bei nafuu kabisa na kila mtu mwenye uwezo wowote wa kiuchumi anaweza kununua aidha kwa kipande kimoja, fungu au hata kwa kilo. Tangawizi inatumikaje? Mmea huu unaweza kuonekana kama wa kawaida na watu kuutumia tu kama mazoea, lakini kiungo hiki kinaweza kutumiwa kama dawa. Kiungo hiki huweza kutumika kikiwa kibichi au kimekaushwa na kutengenezwa unga. Faida zake Tangawizi ni mmea kati ya mimea mingi yenye maajabu, unaweza kutumika kama dawa na kutibu magonjwa mengi tu zaidi ya 72 yaliyo ndani ya miili yetu na kutuacha tukiwa wazima na kutekeleza majukumu yetu ya kila siku. Pia kiungo hiki kinafaida zaidi kwa wagonjwa hasa walio athirika na ugonjwa wa Ukimwi. Hivyo, kwa wale wenye matatizo kama haya wanaweza kupata faida zaidi ya maajabu ya mmea huu. Jinsi ya kutumia kama dawa Tangawizi ikiwa imesagwa au mbichi iliyopondwa pondwa inaweza kutumika kama kinywaji kama ilivyozoeleka kwa watu wengi. Namna rahisi ya kuitumia ni katika chai, inakuwa ni mbadala wako wa majani yale meusi ya chai ambayo yenyewe huwa na kaffein inayosababisha magonjwa mengi mwilini. Pia inaweza kutumika katika vyakula hasa nyama na mbogamboga zingine, inaweza kuongezwa katia juisi freshi pia na kuleta radha nzuri ambayo ni dawa pia. Hutibu magonjwa gani? Tangawizi inaweza kukusaidia kuongeza hamu ya kula, kupunguza kichefuchefu kutapika, kuharisha, kisukari, shinikizo la damu, kuongeza msukumo wa damu na kutoa sumu mwilini. Matatizo mengine yanayoweza kuondoka kwa kunywa tangawizi ni maumivu ya tumbo na gesi tumboni. Pia husaidia uyeyushwaji wa chakula tumboni. Vilevile husaidia kutuliza au kuondoa kabisa mafua au flu na magonjwa mengine mengi. Mwandishi wa makala hii ni tabibu wa tiba asilia, kwa maswali na ushauri wasiliana naye kupitia WhatsApp +255769142586. | 3 |
Mwandishi wetu, Tanga MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema kampeni ya elimu kwa mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) itawasaidia wafanyabiashara wanaokwepa kodi kuacha vitendo hivyo vya kuikosesha Serikali mapato. Shigela ameyasema hayo ofisini kwake alipotembelewa na maafisa wa TRAwanaofanya kampeni hiyo mkoani humo ambayo imelenga kuwaelimishawafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati. Amesema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi pengine kwa kujua au kutokua, jambo ambalo linahitaji elimu ya uelewa ili kila mwananchi afahamu wajibu wake kwenye ulipaji wa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Akiizungumzia kampeni hiyo, Shigela ameipongeza TRA kwa kuendesha zoezi hilo katika mikoa mbalimbali na kusema litaongeza ukusanyaji wa mapato baada ya wafanyabiashara kuelimishwa na kufahamu kuwa maendeleo ya nchi yanasababishwa na ulipaji wa kodi kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, barabara, umeme na maji. Shigela amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanalipa kodi kwa hiari bila kusubiri kubugudhiwa na serikali, huku akieleza kuwa serikali itaendelea kupambana na wakwepa kodi wanaoingiza bidhaa za magendo nchini kwa kupitia bandari bubu zilizopo kandokando ya Bahari ya Hindi. “Nchi yoyote haiwezi kupiga hatua ya maendeleo bila wananchi wake kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa sababu kodi ndio kila kitu huwezi kujenga barabara kama wafanyabiashara hawataki kulipa kodi, huwezi kuimarisha huduma za afya kama hakuna kodi na pia huwezi kuimarisha mifumo ya elimu bila kodi,” alisema Shigela. Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Tanga, Specioza Owure amesema kuwa, maafisa hao wa TRA wanaofanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi, watafika maeneo mbalimbali yenye wafanyabiashara katika mkoa wa Tanga na watawaelimisha kuhusu umuhimu wa kodi na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. “Maafisa hawa wanatumia jitihada zote kuwaelimisha wafanyabiashara, tunafanya hivi ili kila mmoja afahamu wajibu wake wa kulipa kodi sambamba na kusogeza huduma za TRA karibu na wateja,” alisema Owure.Kampeni ya elimu kwa mlipakodi mkoani Tanga inatarajia kumalizika Juni 30, 2020 ambapo lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara, kusikiliza maoni na changamoto zao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. | 5 |
Simba ambao wamebakiza michezo sita, wanatarajiwa kucheza mchezo wao wa ligi dhidi ya Kagera Sugar wiki ijayo kwenye uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga amba po wamepania kuondoka na ushindi wa pointi tatu.Akijibu maswali ya waandishi wa habari juzi msemaji wa Simba, Haji Manara alisema mbio za ubingwa wa ligi ni kama marathoni, na kwamba lolote linaweza kutokea na kubadilisha msimamo wa ligi.“Mbio za ubingwa ni kama marathoni, kwani anayevuka kamba ndiye mshindi, na sisi bado tuko kwenye nafasi nzuri ya kuelekea huko, kwani tunaweza kufanya lolote,” alisema.Manara alitolea mfano wa mwaka 2004 ambapo Yanga na Mtibwa zilikuwa zikiongoza na wao walikuwa hawako katika nafasi nzuri lakini timu hizo zikajikuta zikipoteza michezo kadhaa, na wao wakafanikiwa kuondoka na taji la ligi.Alisema kama ilivyotokea mwaka huo, hata sasa inawezekana kwani hawajakata tamaa kiasi cha kukubali kiurahisi kuwa hawawezi kuchukua taji na kwamba wanajiamini.Msemaji huyo alisema ikitokea wakashindwa kuchukua taji hilo sio kwamba ndio mwisho wa dunia kwani watajipanga zaidi kwa msimu ujao.Simba kwa sasa inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 32 nyuma ya mabingwa watetezi Azam Fc wenye pointi 36 na vinara wa ligi Yanga wenye pointi 37.Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuanza kambi leo kisha kuondoka kati ya kesho au Jumanne kuelekea Shinyanga kujiandaa na mchezo huo dhidi ya Kagera. | 4 |
JAJI Mkuu mstaafu Othman Mohamed Chande amesema kuwa migongano ya maslahi ni ishara ya hali ya hatari, hivyo lazima idhibitiwe, isimamiwe na ibainishwe kwa namna moja au nyingine kwani ina uwezo mkubwa wa kuipa sifa mbaya serikali, sekta za umma, taasisi, viongozi na watendaji.Alisema hayo wakati akizindua mjadala wa maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu kitaifa mjini hapa. Wakati Jaji Mkuu mstaafu akisema hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, George Mkuchika amekiri miongoni mwa masuala ambayo wanapambana nayo ni mgongano wa maslahi. Waziri Mkuchika alisema kwamba jambo hilo bado ni changamoto kubwa hususan kwenye halmashauri nyingi nchini hasa pale linapokuja suala la zabuni.“Utakuta diwani haruhusiwi kufanya kazi kwenye halmashauri lakini anakwenda kuanzisha kampuni anahakikisha anasimamia kupata zabuni, zabuni inatoka kwa haraka pengine analipwa zaidi ya mkataba na anaweza kulipwa hata kama kazi haijamalizika,” alisema.Alisema mambo kama hayo yamekuwa hayaleti picha nzuri hasa pale linapokuja suala la utawala bora. Hata hivyo alisema Tanzania inafanya vizuri katika suala la utawala bora. “Tumejitahidi kupambana na rushwa, pia kati ya nchi 54 katika utawala bora tuko nchi ya 14, lazima tujitahidi,” alisema. Akifafanua zaidi Jaji Mkuu mstaafu Chande alisema mapambano dhidi ya migongano ya maslahi bado yapo na inaendelea ulimwenguni kote.Alisema kuwa uelewa ,utambuzi na uchambuzi makini wa mgongano wa maslahi kwa viongozi na watumishi lazima uzingatiwe kwani moja ya chimbuko lake muhimu ni maadili, pili utumishi wa umma kama jukumu.Alisema kuwa changamoto kwenye maadili, haki za binadamu,vita dhidi ya rushwa ni kutambua kutawala na kudhibiti mapema migongano ya maslahi kwa njia ambayo italingana kulinda maamuzi ya vitendo kutokana na kushawishiwa visivyo. “Wakati mwingine viongozi wa umma lazima mkubali kujivua nyadhifa mlizonazo ili kulinda heshima yenu ,lazima tukubali kuwa kuna maisha baada ya uongozi,” alisema.Vilevile alisema kuwa baadhi ya viongozi wa umma wamekuwa wakishindwa kuwa na maamuzi mazuri katika kutekeleza majukumu yao kwa manufaa binafsi hali inayokiuka maadili na hali za binadamu.Kwa upande wake mtoa mada katika mdahalo huo kutoka Chuo Kikuu cha Biashara Dodoma (CBE), Mhadhiri Godfrey Ngh’umbi alisema kuwa mgongano wa maslahi katika utumishi wa umma unapaswa kufanyiwa tathmini kwa mapana ikiwa ni pamoja na kukabiliana na tatizo sugu la rushwa. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), James Jesse alieleza kuwa kashfa nyingi zinazowakumba baadhi ya viongozi wa umma zinasababishwa na mgongano wa maslahi. | 3 |
Kufuatia kukamilisha dili la aliyekuwa mshambulaji wa TP Mazembe, Deo Kanda, Msemaji wa Mabingwa wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara Simba SC, Haji Manara amesema kuwa sasa ameanza rasmi mazoezi ya kuyatamka majina mbalimbali ikiwemo ya wachezaji wa Kibrazil ambao wamesajiliwa na Simba msimu huu. Manara amewakejeli watani zao kwamba kama anawaona namna wanavyohaha kutokana na namna usajili wao ulivyokuwa kabambe. “Nishaanza Mazoezi ya kuyatamka hayo majina ya kina Romario,sijui Frequelis na haya ya kifaransa ,vinginevyo Simba day ntapuyanga!! Okey Deo Kanda ni fujo zisizoumiza!! ( in voice of @nickbongozozo )
Hahahahaha naviona Vimajimaji vya jamaa hv sasa , ashua zote tepetepe,” ameandika Manara kwenye ukurasa wake wa Instagram. Simba wamewasajili Wabrazil watatu ambao ni mshambuliaji Wilker Henrique da Silva, kiraka Gerson Fraga Viera na beki Tairone Santos da Silva Nishaanza Mazoezi ya kuyatamka hayo majina ya kina Romario,sijui Frequelis na haya ya kifaransa ,vinginevyo Simba day ntapuyanga!! Okey Deo Kanda ni fujo zisizoumiza!! ( in voice of @nickbongozozo ) Hahahahaha naviona Vimajimaji vya jamaa hv sasa , ashua zote tepetepe 😂 A post shared by Haji S. Manara (@hajismanara) on Jul 2, 2019 at 6:07am PDT | 4 |
KIUNGO wa KMC FC, Ally Msengi amesema amefurahi kusajiliwa na klabu ya Stellenbosch ya Afrika Kusini na kudai changamoto mpya zitamsaidia kumjenga. Msengi amesajiliwa na Stellenbosch ambayo inashiriki ligi kuu ya nchini humo kwa mkataba wa miaka mitatu. “Ninafurahia kwenda kuanza changamoto mpya nje ya Tanzania na ninaamini zitanijenga badala ya kuendelea kubweteka hapa nyumbani,” alisema Msengi. Msengi ambaye alikuwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya U17 kilichofuzu kucheza fainali za Gabon 2017 amefanya vizuri akiwa na klabu ya KMC aliyoichezea kwa msimu mmoja na nusu pia amekuwa katika kikosi cha timu ya Taifa U20 Pia ameushukuru uongozi wa KMC kwa ushirikiano mkubwa tangu alipotua hapo na kumruhusu kuondoka kucheza soka nje ya Tanzania. Msengi amepelekwa Afrika Kusini na kampuni ya Siyavuma Sports Group, inayosimamiwa na Michael Mwebe ambaye amesema ni muendelezo wao wa kuwapatia fursa ya kucheza soka la nje ya nchi wachezaji Watanzania na walianza na Abdi Banda, Himid Mao, Eliud Ambokile, Yahya Zaydi na sasa Msengi. | 4 |
Alisema kuwa kikosi chake kilicheza vizuri lakini haikuwa bahati kwao kutwaa ubingwa na kwamba mikwaju ya penalti haina mwenyewe na kuongeza kuwa sasa anaelekeza nguvu kwenye Ligi Kuu bara.Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo ambao timu yake ilifungwa kwa mikwaju ya penalti 4-3 Maxime alisema kufikia hatua hiyo kwa wachezaji wake kazi kubwa ilifanyika na hawezi kuwalaumu kwa kukosa penalti kwani hizo hazina mwenyewe.“Wachezaji wamefanya vizuri kwenye michuano hiyo hadi kufikia kucheza fainali siwezi kuwalaumu kukosa ubingwa kwani penalti hazina mwenyewe na hakuna mwalimu anaekaa na kufundisha kupiga penalti,” alisema.Aidha alisema mashindano ndio yamemalizika na kilichobakia sasa ni kujipanga kwa ajili ya kuendelea vyema na Ligi Kuu ya Tanzania bara ambayo timu yake inaongoza kwa pointi 16.Alifahamisha kwamba katika michuano hiyo wachezaji wake wamepata mazoezi ya kutosha ambayo yatawasaidia. “Tumemaliza michuano salama sote tukiwa wazima na hivi sasa ni kuweza kujipanga kwa ligi”, alisema. | 4 |
Na ASHA BANI-DAR ES SALAAM UPANDE wa uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF), chini ya Mwenyekiti anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba, unadaiwa kulamba Sh milioni 369.378 za ruzuku kinyume cha utaratibu. Inadaiwa kuwa fedha hizo zimetolewa ndani ya siku moja katika matawi matatu tofauti ya Benki ya NMB kwa kutumia akaunti ya chama na baadaye kuhamishiwa kwa mtu binafsi. Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF ambaye hatambuliwi na Msajili, Julius Mtatiro, alisema fedha hizo zilitolewa kutoka Hazina na kupelekwa NMB tawi la Temeke. Wakati Mtatiro akidai hayo, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa CUF, Abdul Kambaya, alidai fedha hizo zimetolewa kihalali kama walivyofanya upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad ambao alidai walitoa Sh milioni 80 kupitia Benki ya NBC. Pamoja na hali hiyo, Mtatiro alisema fedha hizo ziliingizwa katika akaunti binafsi ya mtu aliyetambulika katika muamala kwa jina la Mhina Masoud Omary. Alisema kwa niaba ya Baraza Kuu la Uongozi la CUF ambalo limemteua yeye kuongoza, hana budi kuwajulisha wanachama kuwa CUF imeibiwa fedha hizo za ruzuku ambazo alidai zimetoroshwa na watu wasiojulikana. “Fedha hizo zilitoroshwa kutoka Hazina ya Serikali Kuu Januari 5 na kuingizwa kwenye Akaunti ya NMB Tawi la Temeke yenye jina la The Civic United Front ikiwa na akaunti namba 2072300456. “Bodi ya Wadhamini ya CUF ambayo ndiyo msimamizi wa jumla wa masuala ya akaunti za fedha na mali za chama hicho, haijatambua akaunti hiyo na haikuwahi kuidhinisha ipokee ruzuku ya CUF kutoka Serikali Kuu,” alisema Mtatiro. Alisema Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif, ndiye muwajibikaji mkuu wa masuala ya fedha na mali za chama, hivyo haitambui akaunti hiyo na hajawahi kumwandikia Msajili wa Vyama vya Siasa kumpa akaunti hiyo ili iwekewe fedha za ruzuku ya CUF. Mtatiro aliongeza kuwa vikao vya kitaifa vya chama hicho, kwa maana ya Kamati ya Utendaji ya Taifa iliyokutana hivi karibuni kumpitisha mgombea ubunge Jimbo la Dimani, Zanzibar na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, havikuwahi kupitisha uamuzi wowote kwamba fedha za CUF ziwekwe katika akaunti hiyo. “Baada ya kugundua utoroshwaji huo wa fedha za ruzuku ya CUF ambazo ni fedha za umma na zina masharti na taratibu zake katika kutolewa, tumejiridhisha kuwa akaunti ambayo Hazina ya Serikali Kuu wameshiriki kuitumia kutorosha fedha za umma na mali ya CUF, ni akaunti ya CUF ambayo hutumiwa na Wilaya ya Temeke kwa ajili ya kupokea mgawo wa ruzuku kutoka kwa chama Taifa. “CUF kinazo akaunti katika kila wilaya ya kichama, kwa mfano Wilaya ya Kinondoni ya CUF wanayo akaunti ya benki ambayo wanaitumia kupokea fedha zilizoidhinishwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa ya Chama kwa mujibu wa Katiba, Wilaya ya Ilala pia ina akaunti ya namna hiyo, Mtwara na wilaya nyinginezo,’’ alisema Mtatiro. Aliongeza kuwa baada ya watu wanaomsaidia aliyemtaja kwa jina la ‘Bwana Yule’ kuivuruga CUF na kuona kuwa Bodi ya Wadhamini imezuia njama za ufunguaji wa akaunti mpya ya CUF Ilala, wakatumia mbinu ya namna ile ile kwa njia tofauti kwa Temeke. Mwanasiasa huyo aliendelea kueleza jinsi fedha hizo zilivyotoroshwa, kuwa siku mbili kabla ya utoroshaji huo, ulisukwa mpango wa kuwaondoa baadhi ya viongozi wa CUF wa Wilaya ya Temeke kwenye utiaji saini unaoihusu akaunti tajwa. Alisema uondoaji huo ulikwenda sambamba na kuwageuza baadhi ya wateule wa Profesa Lipumba wanaofanya kazi za kukihujumu chama kutokea Buguruni. Mtatiro alisema watia saini wapya walioshiriki ni aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara ambaye ni Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya na mtu mwingine aitwaye Thomas Malima, ambao wote wapo kwenye mgogoro na chama hicho wakipinga kusimamishwa uanachama wao. “Yaani ni kama vile leo hii ruzuku ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) itoroshwe na kuwekwa kwenye akaunti ya NMB ya CCM ngazi ya wilaya huko Kahama. Kisha fedha hizo ziondolewe kwenye akaunti hiyo ya wilaya na kuingia kwenye akaunti ya mwana CCM aliyesimamishwa uanachama na halafu mwana CCM huyo azitoe fedha hizo na kuzipeleka kusikojulikana, hali ingekuwaje?” alisema na kuhoji Mtatiro. FEDHA ZILIVYOINGIZWA Alisema siku moja baada ya NMB na wala njama hao kukamilisha mchakato wa kubadilisha watia saini wa akaunti ya CUF inayomilikiwa na Wilaya ya Temeke, Januari 5 ndipo Hazina ikaweka fedha hizo bila kuchelewa. Mtatiro alisema Hazina walipotorosha fedha hizo, watia saini wapya wa Akaunti ya NMB ya Wilaya ya Temeke waliulizia kiasi cha fedha kilichomo kwenye akaunti hiyo na walifanya hivyo katika tawi la NMB Mandela Road. Alisema siku ya pili yake yaani Januari 6, aliowaita watia saini wakiongozwa na Malima walikwenda katika Benki ya NMB Tawi la Temeke na kufanya mambo mawili, moja ikiwa ni kuhamisha Sh milioni 69, kisha wakahamisha Sh milioni 300 kwenda kwenye akaunti ya mtu binafsi. “Mchezo wote huo umefanyika ‘chapchap’ kama zilivyochotwa pesa za Escrow,” alisema. Akiendelea kueleza, Mtatiro alisema kuwa akaunti ya mtu binafsi iliyotumika kutoroshea fedha hizo kutoka kwenye akaunti ya Wilaya ya Temeke, ni ya NMB yenye namba 41401600207 inayomilikiwa na Mhina ambaye ni Diwani wa CUF wilayani Handeni na kwamba wameeleza kuwa ni mtu wa karibu wa Profesa Lipumba. Alisema wakati fedha hizo zinahamishiwa kwenye akaunti ya Mhina haikukutwa na senti tano. “Na hii ni mara ya kwanza tunashuhudia kuwa fedha za chama zilizotoroshewa kwenye akaunti ya ngazi ya wilaya zinaondolewa haraka na kuwekwa kwenye akaunti ya mtu binafsi,’’ alisema Mtatiro kwa mshangao. Aliendelea kueleza kuwa Januari 9, mwaka huu, akaunti ya Mhina ilikuwa kwenye mchakato mkubwa wa kuondoa fedha hizo kutoka kwenye akaunti hiyo. FEDHA ZILIVYOONDOLEWA Mtatiro akiendelea kuelezea mlolongo wa uondoaji wa fedha kutoka akaunti ya Mhina, alisema alianza kazi ya kuondoa fedha hizo majira ya asubuhi Januari 6, mwaka huu kwa kuanza kuondoa Sh milioni 100 tawi la Magomeni. “Kisha akiwa hapo hapo Magomeni akatoa tena Sh milioni 50 halafu akaelekea tawi la Kariakoo na kutoa Sh milioni 100 na mwisho akiwa hapo hapo Kariakoo NMB akatoa tena Sh milioni 49.5. “Wakati Mhina anazunguka kwenye matawi haya kutoa fedha hizi, jana alipewa ulinzi wa Jeshi la Polisi waliokuwa wamevalia kiraia wakiwa kwenye magari ya CUF na aliambatana na Thomas Malima wakiwa chini ya usimamizi wa watu wengine wawili, Magdalena Sakaya na Abdul Kambaya. “Baada ya kutorosha fedha hizo zote, akaunti ya Masoud Mhina imebakia na Sh 207,907 kama zawadi maana wakati inawekewa Sh milioni 300 haikuwa na hata senti tano,” alisema. Mtatiro alisema kuwa Oktoba 10 mwaka jana, Msajili wa Vyama vya Siasa alimwandikia Mwenyekiti na Katibu wa CUF na kuwajulisha kwamba ofisi yake inasitisha ruzuku ya CUF kwa kile alichokiita fedha hizo ni za umma ambazo zinahitaji usimamizi mzuri katika matumizi yake. “Kwa kuwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ina dhamana ya kugawa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa vinavyostahili na kusimamia uwajibikaji katika matumizi ya fedha hizo, hivyo baada ya tafakuri ya kina aliona ni busara kwanza kusimamisha kwa muda mgawo wa ruzuku. “Katika maandiko kwa vyama, barua ya Msajili ilikuwa na namba yenye Kumb. Namba HA.322/362/14/17,” alisema. Alisema CUF inafahamu tangu Msajili aiandikie barua kusitisha ruzuku ya chama hicho, sasa ni miezi mitano ambapo CUF inadai ruzuku ya Sh milioni 635. Chama hicho pia kinamwomba Rais Dk. John Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Gavana wa Benki Kuu (BOT), Takukuru, Ofisi ya Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali na vyombo vingine vinavyohusika, kuchukua hatua za dharura za kuokoa fedha hizo za umma. Kutokana na yote hayo, Bodi ya Wadhamini ya CUF tayari inakutana na Kamati ya Utendaji ya Taifa kwa kile alichokiita shambulio kuelekeza hatua za kiutawala na kisheria za kuchukua haraka. HAZINA WAJIBU Msemaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Ben Mwaipaja, alikiri Hazina kutoa kiasi cha Sh bilioni 7.16 Julai hadi Novemba mwaka jana. “Sisi kama wizara tuna jukumu la kupeleka fedha hizo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na si kupeleka moja kwa moja kwenye vyama, Msajili yeye ndiye anayejua mgawanyo wake, hivyo hatuhusiki kwa hilo,’’ alisema Mwaipaja. KAMBI YA LIPUMBA Wakati hayo yakiendelea, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma, Kambaya, alisema hawana sababu ya kumjibu Mtatiro na genge lake, bali kwa kuwa kumeibuliwa hoja inayohusu viongozi halali, wanaona umuhimu wa kutoa ufafanuzi. Alisema CUF inaongozwa na utaratibu wake ikiwamo Katiba, na kama anaona ni kiongozi wa kitaifa, ni vema awasilishe malalamiko yake katika vikao vya chama badala ya kulalamika kwenye vyombo vya habari. “Katibu Mkuu wa chama hiki ni Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti ni Profesa Ibrahim Haruna Lipumba. Ni kweli CUF tumeomba fedha zetu za ruzuku ili ziweze kutusaidia kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 20 kwa upande wa Tanzania Bara. “Ni vyema Watanzania wakafahamu kwamba kupitia kwa Shaweji Mketo, upande wa Maalim Seif Sharif Hamad umetamka bayana kwamba haujasimamisha mgombea kwenye kata yoyote katika uchaguzi huu mdogo unaotarajiwa kufanyika Januari 22, mwaka huu. “Kwa upande wa Bara, CUF tumesimamisha wagombea kwenye kata 14 kati ya 20 zinazopaswa kurudia uchaguzi. CUF ni chama cha wananchi, hatuwezi kuacha kusimamisha wagombea na kuamua kuunga mkono wagombea wa Chadema kama ilivyoelekezwa na Katibu Mkuu kupitia Shaweji Mketo,’’ alisema Kambaya. Alikiri kutolewa kwa fedha hizo ambazo ziliingizwa kwenye akaunti ya chama ambazo sasa zinatumika kwenye shughuli ya uchaguzi wa marudio. “Mbona sisi hatujatoka mbele ya umma na kulalama hatua ya Maalim Seif Sharif Hamad na wale wanaojiita genge mbona si wa kweli, waeleze basi Oktoba mwaka jana walivyotoa Sh milioni 86 kupitia Benki ya NBC bila kuhusisha upande kupitia Naibu Katibu Mkuu Bara Magdalena Sakaya ambaye ni mmoja wa watia saini kwenye akaunti hiyo. “Sisi hatukuona shida pamoja na kutojulishwa kwa kuwa tunajua kuwa fedha zimekwenda kwenye Uchaguzi wa Jimbo la Dimani. Mtatiro hawezi kuyafahamu haya kwa kuwa si kiongozi wa chama hiki,’’ alisema Kambaya huku akiwataka wana CUF kupuuza kelele hizo. | 3 |
Na MWANDISHI WETU AGOSTI mwaka huu, Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo, kupitia huduma yake ya Tigopesa, walitoa gawio la Sh bilioni 2.35 za faida kwa wateja wao wanaotumia huduma hiyo kupitia simu za mkononi. Hii ni robo ya malipo ambayo kampuni imechangia kwa wateja wake, ambapo inakamilisha jumla ya Sh bilioni 81.8 tangu kampuni hii ilipoanza kugawa faida kwa wateja wake mwaka 2014. Suala hili linapotazamwa kwa mtazamo wa kibiashara, utoaji wa faida kwa wateja unaweza kuonekana kama gharama katika biashara hivyo kuwa ni jambo linalopaswa kuepukwa. Wakati huo huo, ni sawa kwamba mteja aliyeridhika ambaye pia kimsingi ndio uti wa mgongo wa biashara anapaswa kuzawadiwa. Mteja yuko katika msingi wa mapato, riba na uvumbuzi unaopatikana katika ngazi ya mabadilliko. Kwa hiyo mteja anapaswa si tu azawadiwe kwa kuamini huduma anazotumia, lakini pia anapaswa kujihisi kuwa yeye ni sehemu ya kampuni kwa kupitia juhudi za kampuni za kutambua mchango wao, na zaidi kwa kujenga kipengele muhimu kinachotakiwa zaidi cha uaminifu wa mteja na kuthamini nembo ya kampuni. Pia inajenga mazingira ya faida ya pande zote ambazo ni kampuni na mteja. Mara nyingi ni tumaini la kampuni nyingi kuongeza uzalishaji, pia wakiwa wanatoa mapato yao kwa njia sahihi na inayoeleweka. Akitangaza riba ya robo mwaka jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo, Simon Karikari, anasema: “Riba ya robo mwaka inadhihirisha zaidi kwamba Tigopesa ni zaidi ya pesa – Tigopesa ‘ni zaidi ya pesa’. Kila robo ya mwaka tunatoa riba ya robo mwaka kwa wateja kwa kutegemea salio lao la kila siku katika akaunti zao za simu za mkononi.” Kwa sasa Tigo wanajivunia mtandao unaokua kwa kasi zaidi nchini wenye zaidi ya wateja milioni 12 waliosajiliwa, zaidi ya wateja milioni saba wanaotumia huduma za kifedha kupitia simu za mkononi, Tigopesa, pamoja na mtandao wa zaidi ya wafanyabiashara 40,000 na ina mawakala 85,000 wa huduma za fedha kupitia simu za mkononi. “Tigo imekuwa ni kampuni ya kwanza ya simu za mkononi duniani kutoa faida yake inayopatikana kutoka katika akaunti ya fedha kupitia simu za mkononi. Tangu mwaka 2014 kampuni imeweza kutoa zaidi ya Sh bilioni 81.8 katika riba ya robo mwaka kwa wateja wake,” anasema Karikari na kuongeza: “Hii ni mara ya 17 mfululizo ambapo Tigo imechangia riba kwa wateja. Ambao kila mmoja anapokea malipo kutegemeana na thamani ya fedha za kielektroniki walizozihifadhi katika akaunti zao za Tigopesa kuendana na matakwa ya Benki Kuu ya Tanzania.” Anasema: “Utoaji huu wa faida ni kwa watumiaji wote wa huduma ya Tigopesa ikiwamo wateja binafsi, mawakala wa rejareja na washirika wetu wa kibiashara wote kwa kutegemeana na thamani ya fedha za kielektroniki zilizoko katika akaunti zao za Tigopesa.” Wakati wote huo, kampuni imeweza kutoa jumla ya malipo yanayokaribia kufika thamani ya bilioni 50 kwa watumiaji wa huduma ya fedha kupitia simu za mkononi na kampuni haitaacha kuhakikisha mapato hayo yanawakilisha hali ya faida kwa wote. Tigo Tanzania imeamua kuhusu utaratibu utakaotumika kutoa faida miongoni mwa wateja kutoka kwenye utoaji wa faida kutegemeana na salio la kila siku la wateja wa Tigopesa kuendana na waraka wa Benki Kuu ya Tanzania iliyotolewa Februari 2014. “Tunashauku kubwa ya kutangaza ongezeko hili la gawio la faida kwa mara ya tisa mfululizo. Jambo hili linadhihirisha utayari wetu wa kutoa nafasi ya kufikia huduma za kifedha kwa wateja wetu nchi nzima kwa ujumla kupitia huduma zetu za Tigopesa,” anasema Karikari. Hali ya soko iliyoboreshwa na ongezeko imara la idadi ya watumiaji wa Tigopesa ni sehemu ya vichocheo vya ongezeko la gawio la faida hususani kutoka kwenye sekta ya wafanyabiashara. Kwa sasa Tigopesa inamtandao mkubwa zaidi wa wafanyabiashara na mawakala nchi nzima. Karikari anabainisha kwamba uwekezaji mkubwa wa Tigo katika upanuzi, uvumbuzi unaolenga mteja, teknolojia ya kidigitali ya kisasa na huduma nzuri kwa wateja imekuwa ni kichocheo kikubwa cha ongezeko la watumiaji na kutumia huduma ya fedha kwa njia ya simu za mkononi. “Tigopesa imeweka juhudu katika agenda ya ushirikishwaji wa kifedha ya Serikali na inatengeneza zana mpya za kibiashara za kidigitali na kuandaa mazingira kuelekea katika mtindo wa maisha usiotumia fedha taslimu, kwa kupanua mfumo wake wa kifedha na kiuchumi, kuboresha ubora wa huduma zake na kutambulisha njia za kibunifu, zenye ufanisi kwa ajili ya wateja kufurahia huduma bora zaidi,” anaongeza Karikari. | 0 |
Khamis Sharif -Kusini Unguja UONGOZI wa Shule ya Sekondari Paje Wilaya ya Kusini Unguja, umemuhamisha shuleni hapo mwanafunzi wa kiume ambaye anadaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi mwenzake. Akithibitisha uhamisho wa mwanafunzi huyo, mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Issa Abdallah Makame alisema kuwa uongozi huo umeridhia hatua hiyo kwa lengo baada ya kuona ukubwa wa tatizo hilo shuleni hapo. Alisema suala la wanafunzi kumpa ujauzito katika mazingira ya shule hiyo ni geni hivyo, uongozi umefanya uamuzi huo mgumu iki kutaka kuona matendo hayo hayajirejei tena kwa wanafunzi shuleni hapo. Alisema kuwa mwanafunzi huyo ambae jina lake limehifandhiwa anasoma kidato cha nne na tayari ameshapewa taarifa za kutafuta skuli nyengine ili kuendelea na masomo yake mara shule zitakapofunguliwa. Aidha mkuu huyo wa shule alisema kuwa mwanafunzi huyo anadaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi mwenzake ambae anasoma kidato cha tatu shuleni hapo. “Tulichokifanya kwanza ni uchunguzi yakinifu na ndipo tukaamua kukutana na kukubaliana tumpe uhamisho na ulikuwa tumpunzishe moja kwa moja lakini kwa vile karibuni anafanya mtihani ni bora aende akamalizia katika skuli nyingine kwani kuendelea kubakia hapa kutawafanya na wengine kuiga na kuishi kwa woga. “Hii ni hukumu yetu kama shule tu, bila shaka kuna hukumu nyingine ya familia ya mtoto wa wa kike huko sijui itakuwa ipi kwani sio suala rahisi mzazi kufanyiwa mtoto wake kitendo kama hiki kisha wakamuangalia tu,” alisema Mwalimu Abdallah Alisema tukio hilo ni la kwanza kwa wanafunzi kupeana ujauzito lakini wameona ni bora kuchukua hatua haraka ili wengine wasireje. Akizungumzia hilo, Mratibu wa Wanawake wa Shehiya ya Paje, Asya Mussa Dai, alisema kuwa uamuzi waliochukuliwa na uongozi wa shule si mbaya kwani litakuwa fundisho kwa wengine. | 3 |
Na ARODIA PETER -DAR ES SALAAM
JUKWAA la Katiba Tanzania (Jukata), limemwandikia barua Rais Dk. John Magufuli ya kuomba kukutana naye ili wampe ushauri wa mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Jukata, Deus Kibamba, alisema wanakusudia kumweleza na kumshauri Magufuli umuhimu wa mahitaji ya kupatikana kwa Katiba mpya kuliko wakati mwingine wowote ili imsaidie katika kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
“Pia Jukata inafanya maandalizi ya kuratibu mkutano mkuu wa kitaifa ikiwa ni njia mojawapo itakayotumika kukamilisha mchakato wa Katiba mpya,” alisema.
Kibamba alisema ni zaidi ya mwaka mmoja sasa tangu Magufuli aingie madarakani, lakini hakuna taarifa rasmi ya Serikali kuhusu dira na mwelekeo wa mchakato wa Katiba mpya licha awali kusitishwa ili kupisha shughuli za uchaguzi.
Alisema kwa kipindi hiki ambacho Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2017/2018, ni lazima suala la Katiba lipewe nafasi kwa sababu miaka miwili ijayo nchi itakuwa inajiandaa kuingia katika uchaguzi, ukiwamo ule wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwaka 2019 na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwaka 2020 na hakuna muda mwingine wa kumalizia mchakato huo ulioachwa na Serikali ya Awamu ya Nne.
Pia alisema wanamwomba Magufuli avunje ukimya kwa kuwaeleza Watanzania mwelekeo wa kupata Katiba mpya kabla robo ya kwanza ya mwaka huu haijaisha.
Alisema wao bado wanaamini tamko la Magufuli kupitia hotuba yake alipozindua Bunge mwaka juzi, kwamba anafahamu kuna kiporo cha Katiba mpya kilichoachwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete.
“Kwa maneno yake, ni wazi rais aliahidi kuhakikisha Tanzania inapata Katiba mpya katika kipindi chake cha uongozi, hii itamsaidia katika juhudi zake za kutatua changamoto zinazoikabili nchi.
“Nia yetu ni njema kwamba rais ndiye pekee atakayeondoa mkwamo huu wa Katiba, hivyo tunaamni tukikutana naye tutaweza kujadiliana naye na tutamshauri umuhimu wa mchakato huo na hofu iliyopo miongoni mwa wananchi, huku kila mtu akiishi kwa kubashiri na kujiuliza maswali na wengine wakikata tamaa.
“Unaposema unanyoosha nchi sawa. Lakini hatuwezi kunyoosha nchi kwa kamba au kwa pima maji, nchi inanyooshwa na Katiba. Inawezekana kwamba ni suala la bahati mbaya washauri wa rais kuhusu Katiba na sheria hawajafanya kazi yao sawasawa kuhusu hili,” alisema Kibamba.
Kuhusu mkutano mkuu wa kitaifa, alisema utajumuisha asasi mbalimbali za kiraia, Serikali na wasomi waliobobea katika michakato ya kidemokrasia kutoka nje na ndani na watafanya uchambuzi na kushauri mwelekeo mpya kutoka hapa tulipo. | 3 |
Katika mchezo huo ambao ulishuhudiwa na mashabiki wengi, Goms ilikuwa ya kwanza kupata bao mapema dakika ya tatu lililofungwa na Hamza Alaba.Lakini dakika ya saba Danis David aliisawazishia Itezi bao hilo na dakika ya 20 wakaongeza bao la pili lililofungwa na Salum Upuu na kufanya kipindi cha kwanza kumalizika kwa 2-1.Kipindi cha pili kila timu iliingia ikiwa na kasi na kuanza kushambuliana kwa zamu, lakini Itezi walionekana kuwa na kasi ya mchezo lakini makosa ya kufanya faulo karibu na eneo ya goli yaliwagharimu baada ya Goms kutumia faulo na kusawazisha bao lililofungwa na Chinedu Michael dakika ya 70.Bao hilo liliamsha nderemo kwa mashabiki wa Goms na kuanza kushangilia na kutoa kejeli kwa Itezi, hali iliyowapa nguvu wachezaji wao na kufanikiwa kuongeza bao la ushindi dakika ya 78 lililofungwa na Hamza Alaba.Goms ambao ni washindi wa pili wa mashindano ya Ndondo mkoa wa Dar es Salaam, wanasubiri mshindi kati ya Misosi ambao ni mabingwa wa Ndondo mkoa wa Dar es Salaam na Mnadani ya Mwanza kucheza fainali keshokutwa.Akizungumza baada ya mchezo kumalizika nahodha wa Itezi, Romario Albert alisema mechi ilikuwa nzuri na walitawala mchezo kwa kipindi kirefu lakini walifungwa na kuwaomba wana Mbeya kuendelea kuwasaidia.Nahodha wa Goms, Paul John alisema waliruhusu mabao mawili kipindi cha kwanza kutokana na kuidharau Itezi, hivyo kipindi cha mapumziko kocha alibadilisha mbinu na kufanikiwa kushinda.“Pia aliwataka mashabiki wa Goms kukaa mkao wa kula kwani safari hawarudii makosa kwa sababu mara ya kwanza tuliteleza lakini safari hii wapo vizuri. | 4 |
Na MOHAMED HAMAD-MANYARA WILAYA ya Kiteto ilizinduliwa mwaka 1974, wakati huo kulikuwa na idadi ya watu 12,000, hivi sasa idadi ya watu imeongezeka na kufikia zaidi ya 240,000 kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012. Wakati wilaya inazinduliwa maji yalitosha kulingana na idadi ya watu waliokuwepo na waliweza kufanya shughuli za maendeleo, tofauti na ilivyo sasa ambapo wakazi wengi wanalazimika kutumia muda mwingi kutafuta maji kuliko kufanya shughuli zingine za maendeleo. Hali hii imekuwa tishio kubwa kwa familia na wananchi wa Kibaya hasa wa vijijini ambao vipato vyao vinaishia kununua maji,
huku kukiwa na mahusiano mabaya kati ya wanandoa kufuatia huduma hiyo ambayo inapatikana kwa taabu kubwa. Viongozi wilayani Kiteto wamekuwa wakilalamikiwa kwa kushindwa kusogeza huduma ya maji karibu na wananchi, huku kukiwa na ahadi zisizotimia kuwa Serikali iko mbioni toka kuzinduliwa mwaka 1974 hadi leo 2016. Wilaya hiyo ina uwezo wa kujimudu kwa maji safi na salama kwa asilimia 36 vijijini na asilimia 37 mjini. Pia miundombinu inayotumika bado ni ile ya mwaka 1974 kama matenki na mabomba licha ya jitihada zinazofanywa kubadilisha, zikilenga kuondoa adha hiyo bado hali hiyo imekuwa tishio. Urasimu nao umetajwa kuwa kikwazo cha huduma hiyo ambapo aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk. Ally Mohamed Shein ambaye kwa sasa ni Rais wa Zanzibar, aliwahi kuzindua tanki la lita 300,000 mjini Kibaya na baada ya kuondoka halikuweza kuingiza maji. WANANCHI Asha Issa mkazi wa Kaloleni, anasema wakati mwingine huwa wanapanga foleni kwa siku mbili ili kuweza kupata maji. “Tunaamka alfajiri tunaacha watoto nyumbani kwa ajili ya kwenda kutafuta maji, lakini unaweza kushinda siku nzima na maji usipate kwa sababu foleni inakuwa kubwa…unaweza kupanga foleni siku mbili ndio unapata maji,” anasema Issa. Anaiomba Serikali kuhakikisha inatatua kero ya maji kutokana na ukubwa wa tatizo hilo ambalo linawagharimu na hivyo kushindwa kuendesha maisha yao na familia zao. Naye Elias Kona mkazi wa Kijungu, anasema ndoo moja ya maji katika maeneo ya vijijini huuzwa kati ya Sh 500 mpaka 700 huku maeneo ya mijini ikiuzwa kati ya Sh 100 hadi 300. “Tunashindwa kufikia malengo yetu kwa kutumia muda na fedha nyingi kusaka maji. Hali huwa mbaya zaidi kuanzia Julai hadi Desemba kwani maji huwa machache kutokana na ukame. “Angalau mvua ikinyesha huwa kuna nafuu lakini kiangazi tunapata taabu sana, tunatembea umbali mrefu kutafuta maji na kushindwa kufanya shughuli zetu zingine,” anasema Kona. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Dongo, Elia Dengea (CCM) anasema, kuna kila sababu ya kufanyika utaalamu kwa kina katika maeneo ya Kiteto hasa kata yake ambako walichimba maji zaidi ya mara sita bila mafanikio. “Hali hii imekuwa tatizo kubwa hakuna mwananchi anayemwamini kiongozi, wanasema tutakutana kipindi cha uchaguzi,” anasema Dengea. Naye Diwani wa Kata ya Matui, Kidawa Othman (Chadema), anasema tatizo lililopo ambapo kwa sasa linagharimu wananchi kuhusu sekta ya maji ni kukosa watumishi wa Serikali ambao ni waadilifu akisema kuna hujuma nyingi zinafanyika huku kukiwa hakuna hatua zilizochukuliwa. Anasema katika eneo lake wananchi wanatumia maji ya visima vifupi vya kuchimbwa kwa mkono ambavyo si salama kiafya. Mbunge wa Viti maalumu Manyara, Esther Mahawe (CCM), alilazimika kwenda kumuomba Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe, kuja kutembelea katika Mkoa wa Manyara kujionea hali ilivyo katika upatikanaji wa maji. Anasema, Serikali haina budi kutatua kero ya majini hasa vijijini kwani hali ni mbaya kwa wananchi. “Wananchi wanatumia muda mwingi kutafuta maji kuliko kufanya shughuli zingine za maendeleo. Naibu Waziri umejionea mwenyewe hali ilivyo, tunaomba msaada wako ili kusaidia akina mama wa Kiteto na Manyara wanaotaabika kila kukicha,” anasema Mahawe. Naye mbunge wa Kiteto, Emmanuel Papian (CCM), anaiomba Serikali kuendelea na jitihada za kusogeza huduma za jamii karibu na wananchi ili wananchi wawe na imani na viongozi waliopo madarakani, na kuwasihi wananchi kutunza miradi katika maeneo yao. Anasema kukosekana kwa vyanzo vya maji vya uhakika kumechangia kuwapo kwa uhaba mkubwa wa maji. “Visima vingi vinapochimbwa huwa havitoi maji, tunawaomba wataalamu wa maji waliobobea waje Kiteto kusaidia wananchi ambao wanataabika,” anasema Papian. Kwa mujibu wa taarifa kutoka wilayani hapo, vyanzo vya maji vilivyopo ni visima virefu 74, visima vifupi 8, chemchem 6, mabwawa makubwa 5, mabwawa madogo 36 na matenki ya kuvunia maji ya mvua 80. HALI ILIVYO Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kiteto, Tamimu Kambona, anasema kumekuwa na ongezeko la gharama katika baadhi ya hivyo kuna uhitaji mkubwa wa fedha ili kukamilisha miradi ambayo imekwama na kusababisha wananchi kupata adha kubwa ya maji. Kulingana na Mkurugenzi huyo, baadhi ya miradi ilikuwa inatumia mifumo ya jua na kwamba linapokosekana upatikanaji wa maji huwa mgumu. Anasema lengo la Serikali ni kutekeleza sera ya kuwa wananchi wayafikie maji mita 400 pawe kituo, akisema kwa sasa makusanyo yameongezeka sambamba na kuzuia mianya ya wizi Serikalini hivyo kuna uwezekano mkubwa wa kufikiwa sera hiyo ambayo kila Mtanzania anatufaika nayo. Kwa mujibu wa Kambona, miradi ya maji mjini Kibaya na Kaloleni, imetekelezwa kwa asilimia 75 ambapo kazi zilizofanyika ni
usanifu wa mradi, kufungwa mfumo wa nishati ya jua, kufungwa pampu moja, kulazwa mabomba na kufukiwa mitaro. Mradi mwingine ni wa umwagiliaji uliopo Kijiji cha Orgira Kata ya Sunya, ambao umefikia hatua za mwisho za utekelezaji, uchimbaji wa kisima ulikamilika, ufungaji wa pampu, ulazaji wa mabomba, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji, ujenzi wa kituo cha kunyweshea mifugo, pamoja na ujenzi wa tanki la maji na miundombinu yake. NAIBU WAZIRI WA MAJI Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe, hivi karibuni alitembelea miradi ya maji na umwagiliaji mkoani humo na kusema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ina mkakati wa kumaliza kero za maji katika mkoa huo ifikapo mwaka 2025. | 3 |
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe ameipongeza Kampuni ya Petrobena EastAfrica, kwa kufadhili mradi wa kilimo cha mpunga wa ekari 50 unaoendeshwa na kikundi cha vijana cha AgriAjira wilayani Kilosa.Akizungumza na waandishi wa habari, alipofanya ziara katika shamba la vijana, Dk Kebwe alisema juhudi za kikundi hicho, zitasaidia kuongeza uzalishaji wa mazao na kutengeneza ajira nyingi kwa vijana.“Naipongeza Petrobena kwa kufadhili mradi huu kwa kuwapatia pembejeo za kilimo zikiwemo mbegu, mbolea na elimu bora yakilimo mambo ambayo kwa pamoja yamewafanya kufikia hatua nzuri katika kilimo cha mpunga na kufikia hatua ya kuvuna mpunga safi,” alisema Dk Kebwe.Alisema mradi wa AgriAjira ni ushahidi tosha kwamba kuwekeza vizuri katika kilimo, kutazaa ajira za uhakika kwa asilimia kubwa ya wananchi Tanzania na ambao ni vijana. “Hatua iliyofikiwa katika shamba hili ni nzuri. Sisi kama serikali nitahakikisha viongozi wa wizara vinazohusika na kilimo, biashara na viwanda wanafika katika eneo hili ili wajionee mradi huu na kuwahakikisha soko la mpunga utakaovunwa,” alisema Dk Kebwe.Aliwaomba wadau wa maendeleo kujitokeza kuunga mkono miradi inayoanzishwa na vijana, hasa katika sekta ya kilimo ili kuwatengenezea ajira vijana kupitia miradi yenye tija kiuchumi na kijamii kwa maendeleo ya Taifa. “Serikali ya Awamu ya Tano imejielekeza kujenga uchumi wa kati na wa viwanda ambao msingi wake mkubwa unategemea sekta ya kilimo ambayo huzalisha malighafi ambazo zitachochea uanzishwaji na uendelezaji wa viwanda na kupelekea uchumi wa nchi kukua,” alisema Dk Kebwe. Alieleza kuwa ni lazima kuwekeza katika sekta ya kilimo, ambayo ni mhimili mkuu katika ujenzi wa viwanda na biashara.Aliongeza kuwa nguvu kubwa ielekezwe kwenye kuwajengea uwezo wananchi katika kukifanya kilimo kiwe na tija. Mkurugenzi Mkuu wa Petrobena East Africa, Peter Kumalilwa alisema kampuni yake imejikita katika kushiriki kuendeleza sekta ya kilimo nchini kwa kusambaza mbolea za YARA na pia kutoa elimu na kanuni bora za kilimo ili kukuza uzalishaji mazao nchini.“Tumefadhili mradi huu wa kilimo cha mpunga lengo likiwa kutengeneza ajira kwa vijana na pia kukuza uzalishaji wa mazao ili azma ya serikali ya awamu ya tano kufikia uchumi wa kati na viwanda ifikapo 2025 ifikiwe,” alisema Kumalilwa. | 3 |
Yanga imemsimamisha Niyonzima kwa muda usiojulikana kwa kuchelewa kuripoti kambini baada ya kutoka mapumzikoni. Akizungumza na gazeti hili, jana Dk Tiboroha alisema walikutana na mchezaji huyo na wamekubaliana aandike kwa maandishi ili waweze kutafuta suluhisho.“Klabu inahitaji uwepo wa mchezaji kwenye programu za timu anapohitajika kuondoka kwenda kwenye shughuli zake za timu ya taifa kwa ruhusa lakini pia kurudi kwa muda unaotakiwa kwasababu haya ni ya kanuni za FIFA, kwamba kama ni mechi za kutafuta kufuzu mchezaji anatakiwa afike kabla ya saa 48 na baada ya kuitumikia timu yake ya taifa saa 48 baadae anatakiwa arudi kwenye klabu yake,” alisema Tiboroha.“Sasa inapotokea mchezaji hayupo kwenye timu kwasababu alikuwa kwenye timu ya taifa halafu anakosa mechi za kwenye ratiba ya ligi hicho kitendo tumeona hatuwezi kuendelea kukivumilia lazima tujue sababu yake ni nini na ni lazima tupate maelezo ya kina kutoka kwa mchezaji kwanini achelewe kurudi,” alisema Tiboroha.Mbali na wachezaji wa Yanga kupewa mapumziko kutokana na kusimama kwa ligi Niyonzima pia alikwenda kuitumikia timu yake ya taifa Amavubi iliyokuwa ikishiriki michuano ya kombe la Chalenji Afrika Mashariki na Kati iliyofanyika Addis Ababa, Ethiopia.Huku wenziwe wakiwa wameshaanza kambi na kucheza mechi za Ligi Kuu, Niyonzima alirudi akiwa amefungwa plasta gumu (PoP) mguuni na kudai aliumia kwenye michuano ya Chalenji lakini hilo halikusaidia kukwepa adhabu, alikutana na rungu la Yanga. | 4 |
MREMBO wa vyuo vikuu nchini ya El Salvador, Mariselo De Montecristo ameahidi kujitolea kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania nje ya nchi kwa kuwa bado havijulikani nje ya nchi.Mrembo huyo aliyasema hayo alipokuwa katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire iliyopo mkoani Manyara na kupokelewa na mkuu wa idara ya Utalii ya Hifadhi hiyo, Neema Philipo.Alisema aliposhuka tu katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro, KIA, alijiona yuko katika nchi yenye hali tofauti kimazingira na kila alipokuwa akipata taarifa ya vivutio mbalimbali kutoka kwa muongoza watalii, Denis Meela pale KIA na Tarangire, alijuwa wazi kuwa nchi hii ina vivutio vingi, lakini havijatangazwa nje ya nchi.Montecristo ambaye aliambatana na mama yake mzazi na rafiki yake wa kiume alisema ni mara yake ya kwanza kuja nchini, lakini aliahidi kuwa Balozi mzuri wa kutangaza vivutio katika mji wa Califonia nchini Marekani anakoishi na kufanya kazi.‘’Ni mara yangu ya kwanza kuja hapa Tanzania na nimefurahishwa sana na vivutio vya kitalii nilivyoviona hapa Tarangire na nitakuwa Balozi wa kutangaza vivutio katika mji wa Calfonia ili watalii wengi waweze kuja kutembelea hifadhi hii,’’ alisema.‘’Zawadi za kitamaduni nilizopewa na uongozi wa Tarangire na akina mama wa kimasai ni kichocheo kikubwa kwangu kuutangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi, “alisema mrembo huyo.Mkuu wa Idara ya Utalii katika Hifadhi ya Tarangire, Neema alisema kuja kwa mrembo huyo kutautangaza utalii nje kwani ameahidi kufanya hivyo baada ya kujionea mwenye vivutio kibao katika hifadhi ya Tarangire ukiachilia mbali wanyama.Neema alisema ameahidi kutembelea hifadhi mbalimbali hapa nchini ikiwemo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na kupiga picha, lengo ni kuutangaza utalii nje ya nchi.Muongoza Watalii Meela alisema kuwa mrembo huyo amevutiwa sana na vivutio vingi vya hapa nchini na alipokuwa akimpa taarifa za vivutio hivyo alisema angependa kwenda kila sehemu ya vivutio hivyo.Meela amesema, mrembo huyo ameahidi mambo mengi, ikiwemo kuutangaza utalii nje hasa Calfonia anakoishi na ameahidi kuwahimiza warembo wengi zaidi wa nchi mbalimbali kuja nchini kutalii. | 4 |
Na MOHAMED KASSARA -DAR ES SALAAM KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, leo kitakuwa na kibarua kizito cha kusaka ushindi dhidi ya Benin katika mchezo wa kimataifa wa kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa). Stars itaingia katika mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Malawi katika mchezo kama huo uliochezwa Oktoba 7 kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Matokeo ya mchezo huo yaliifanya Stars kushuka kwa nafasi tano katika viwango vya ubora vilivyotolewa na Fifa Oktoba, ikitoka nafasi ya 120 hadi 125. Mchezo huo utakuwa wa kwanza wa kirafiki kwa Stars kucheza ugenini, tangu kocha Salum Mayanga alipokabidhiwa jukumu la kuinoa timu hiyo Januari 2, mwaka huu, akirithi mikoba ya mtangulizi wake, Boniface Mkwasa. Mayanga ameiongoza Stars kucheza michezo minne ya kirafiki nyumbani bila kupoteza, dhidi ya timu za Botswana (mara mbili), Burundi na Malawi, akishinda mitatu na kutoka sare moja. Kocha huyo pia ameweka rekodi ya kuiongoza Stars kucheza jumla ya michezo 13 tangu achukue jukumu hilo, akishinda mitano, sare sita, huku akipoteza mmoja dhidi ya Zambia. Stars ilisafiri usiku wa kuamkia Alhamisi kwenda Benin na kikosi cha wachezaji 21. Kuelekea mchezo huo, Mayanga alifanya mabadiliko madogo ndani ya kikosi chake, akiwaacha beki Erasto Nyoni na kiungo Mzamiru Yassin ambao walilimwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Malawi na kuwajumuisha na Jonas Mkude na Mudathir Yahya. Katika mchezo huo, Stars itamkosa nahodha wake, Mbwana Samatta ambaye ameshindwa kujiunga na kikosi hicho kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti aliyoyapata wakati akitumikia klabu yake ya KRC Genk katika mchezo wa Ligi Kuu ya Ubelgiji. Kukosekana kwa Samatta ambaye ndiye kiongozi wa safu ya ushambuliaji, kuna maana jukumu hilo sasa litaongozwa na Simon Msuva anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya Diffa El Jadid inayoshiriki Ligi Kuu nchini Morocco. Kwa upande wa Benin, itaingia katika mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kulazimisha bao 1-1 dhidi ya Congo Brazzaville katika mchezo wao uliopita. Leo Benin itashuka dimbani ikihitaji ushindi ili kulipa kisasi cha kupokea kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa Stars katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Oktoba 12, 2014 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mabao ya Stars siku hiyo yalifungwa na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ aliyekuwa nahodha, huku mengine yakiwekwa kambani na Amri Kiemba, Thomas Ulimwengu na Juma Luizio, bao la kufutia machozi la Benin likifungwa na Suanon Fadel. Akizungumza na MTANZANIA jana, Mayanga alisema anaamini wachezaji waliopo kwenye kikosi hicho watajituma na kushinda mchezo huo bila ya uwepo wa Samatta. Mayanga alisema wamepanga kucheza kwa nguvu ili kupata ushindi ambao ndiyo kiu ya Watanzania, lakini pia kumfariji Samatta ambaye ripoti ya daktari wa Genk inadai atakuwa nje ya uwanja kwa wiki sita. “Lazima nikiri kuwa Samatta ni mchezaji muhimu kwenye kikosi changu na kukosekana kwake kuna vitu tutavikosa, lakini nina matumaini ya kupata ushindi kupitia wachezaji waliopo,” alisema Mayanga. | 4 |
TIMU ya Mbao imesema inajua kasi ya wapinzani wao Simba kwa sasa hivyo, inajipanga kuendana nao ili kuwadhibiti katika mchezo wa Ligi Kuu utakaochezwa mwishoni mwa wiki hii.Mchezo huo utakuwa ni mtihani kwa Kocha Salum Mayanga aliyekabidhiwa timu hivi karibuni kuchukua mikoba ya Ally Bushiri baada ya kushindwa kufanya vizuri. Akizungumza na gazeti hili jana, Mayanga alisema mchezo wa Simba hautakuwa rahisi kwa sababu wako vizuri, lakini haiwafanyi kuwahofia zaidi ya kujipanga kuendana sawa.“Simba ipo kwenye kasi, ina wachezaji wazuri na tunawaheshimu tukiendelea kujipanga kuhakikisha tunapata pointi tatu,” alisema na kuongeza kuwa wakati wowote wataingia Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo huo. Alisema mchezo huo unaweza kuwa mgumu kutokana na kwamba wanakutana na timu yenye kiwango cha juu inayoshika nafasi ya tatu katika michezo 21 ikiwa na pointi 54.Mayanga alisema anaamini kwa aina ya kikosi alichonacho kitafanya vizuri na kurudi katika kiwango chake. Alisema muhimu ni wachezaji wake kuzingatia nidhamu na kufuata maelekezo wanayopewa ikiwemo kujituma.Mbao imekuwa ikishuka siku hadi siku ambapo katika michezo 30 iliyokwishacheza, imeshinda tisa, sare tisa na kupoteza 12, ikifikisha pointi 36 katika nafasi ya 14. Iwapo itapoteza mchezo huo itazidi kujiweka hatarini ikiwa wengine waliofanana pointi na kutofautiana kidogo watashinda. Hata hivyo, katika mchezo wa raundi ya kwanza uliochezwa jijini Mwanza, Mbao iliibuka na ushindi wa bao 1-0 hivyo, huenda Simba ikataka kulipiza kisasi. | 4 |
WAKULIMA wa zao la korosho Mkoa wa Lindi bado wanadai Sh bilioni 6.5 za msimu uliopita wa mwaka 2018 kutoka Benki ya Wakulima (TADB).Mrajisi msaidizi wa vyama vya msingi vya ushirika Mkoa wa Lindi, Robert Nsunza aliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye kikao cha kujadili msimu wa zao la korosho wa kuanza kwa minada kilichowashirikisha viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika, wenyeviti wa halmashauri za wilaya, kamati za ulinzi na usalama, wataalamu kutoka taasisi mbalimbali.Alisema kati ya fedha hizo, Sh bilioni 3.4 za wakulima wa wilaya ya Nachingwea, mkoani humo. Nsunza alisema Wilaya ya Liwale wanadai Sh bilioni 1.8, Ruangwa wanadai Sh milioni l.75, Lindi Mjini Sh milioni 200 na wilaya ya Mtama Sh milioni sita hivyo jumla ni Sh bilioni 6.5. Aidha serikali ilishatoa ahadi kuwa watalipwa haki zao hizo mwezi huu kutoka TADB.Alisema kwamba msimu uliopita ulikuwa na mtikisiko wa soko, hali ambayo ilisababisha serikali kukusanya korosho kwa wakulima kupitia bodi ya mazao mchanganyiko. Naye Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Hassan Masala alisema wakulima wake wanadai fedha zao Sh bilioni 3.4, madai ya wakulima 3,000 za msimu uliopita.Mkuu wa Mkoa Lindi, Godfrey Zambi alikiambia kikao hicho kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe na Mkurugenzi wa TADB waliahidi fedha za wakulima wa zao hilo la korosho watalipwa mwezi huu. | 3 |
NA THERESIA GASPER, DAR ES SALAAM MAKOCHA wa timu za Simba na Mgambo Shooting, Jackson Mayanja na Bakari Shime, kila mmoja ametamba kutoka na ushindi katika mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara mzunguko wa pili utakaochezwa kesho Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Simba inakutana na Mgambo ikiwa na kumbukumbu ya kuifunga mabao 2-0, katika mchezo wao wa mzunguzo wa kwanza Uwanja wa Mkwakwani, lakini pia mchezo uliopita Simba ilifanikiwa kutoa kichapo cha mabao 4-0 dhidi ya African Sports mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, wakati Mgambo walitoa sare ya bao 1-1, dhidi ya Ndanda FC Tanga. Akizungumza na MTANZANIA, Mayanja ambaye ni mwenyeji wa mchezo huo alisema hawezi kuidharau timu hiyo ila atakuwa makini kuhakikisha wanawakabili wapinzani wao Mgambo Shooting. “Katika mchezo lolote linaweza kutokea, hivyo hatuwezi kubweteka badala yake tutaendelea kujipanga ili kupata matokeo mazuri kwenye mchezo huo. “Hatuwezi kuidharau timu yoyote hata kama ndogo kwa sababu zote zinashiriki Ligi Kuu, hakuna anayetaka kupata matokeo mabaya tutaendelea kufanya vizuri ili kuzidi kupanda juu zaidi,” alisema. Alisema wanaendelea na mazoezi ili kuyafanyia kazi mapungufu aliyoyaona kwenye mchezo uliopita yasijirudie tena kwenye mchezo huo unaowakabili mbele yao, huku wachezaji wake wakizidi kumpa matumaini kutokana na kufuata yale ambayo anawaelekeza kufanya na kuzidi kufanikiwa kupata matokeo mazuri. Kwa upande wake, Shime amesema licha ya timu yake kucheza ugenini, hawatakuwa tayari kuona wanapoteza mchezo huo. Alisema watahakikisha wanapambana kwenye mchezo huo ili waondoke na pointi tatu muhimu. “Matokeo mazuri yanapatikana popote pale, sio kama unapocheza ugenini mchezo ndio unakuwa mgumu si kweli, sisi tumejiandaa kwenye mazingira ya kuchezea popote pale na sasa tupo njiani kuelekea Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo,” alisema. Alieleza Simba ni timu kubwa, lakini haiwezi kuwazuia wao kufanya vizuri kutokana na alivyokiandaa kikosi chake ambapo ameyafanyia kazi mapungufu yaliyokuwa kwenye kikosi. Mpaka sasa Mgambo Shooting inashikilia nafasi ya nane huku ikiwa imejikusanyia pointi 17 sawa na Toto Africans zikiwa zimetofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungana. | 4 |
['Tottenham wamefikia makubaliano na Juventus kuhusu uhamisho wa mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala, 25, kwa dau la karibu £62m. (Sky Sports Italia, via Daily Mail)', 'Dybala anajiandaa kuanza mazungumzo ya mkataba na Tottenham kabla ya Alhamisi ambao ni muda wa mwisho uliowekwa kwa uhamisho wa wachezaji kukamilika. (Goal)', 'Tottenham pia wanapania kumsaini mshambuliaji wa Barcelona wa miaka 27- Mbrazil Philippe Coutinho. (ESPN)', 'DC United wanajiandaa kufanya mazungumzo na wawakilishi wa kiungo wa kati wa Arsenal Mesut Ozil, 30, wanapojaribu kujaza pengo lililoachwa wazi na Wayne Rooney anayeelekea Derby. (Mirror)', 'Manchester United wameongeza juhudi ya kufikia mkataba na na kiungo wa kati Tottenham Christian Eriksen, 27. (Telegraph)', 'Eriksen hayuko katika mpango wa wa muda mrefu wa Mauricio Pochettino, Tottenham - na tayari amethibitisha kuwa anataka changamoto mpya. (Mirror)', 'Uamuzi wa dakika za mwisho wa United kumhusu Eriksen unakuja licha ya tetesi ikiwa kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, ataendelea kuwa katika klabu hiyo hadi mwisho wa dirisha la uhamisho litakapofungwa. (Standard)', 'United pia wanawatarajiwa kufanya uamuzi ambao haukutarajiwa kumnyakua mshambuliaji wa zamani wa Tottenham Fernando Llorente, ambaye kwa sasa yuko huru kuondoka klabu hiyo bila malipo. (Sky Sports Italy, via Metro)', 'Manchester City wanatarajiwa kuthibitisha usajili wa Joao Cancelo kutoka Juventus siku ya Jumatano baada ya beki huyo wa miaka 25 raia wa Ureno kupita vipimo vya kimatibabu. (Star)', 'Liverpool hawana mpango wa kumuuza kiungo wa kati wa Brazil Fabinho, licha ya tetesi zinazomhusisha mchezaji huyo wa miaka 25 na uhamisho wa Real Madrid. (Echo)', 'Crystal Palace wamekataa ofa ya £70m kutoka kwa Everton kumnunua mshambuliaji wa Ivory Coast forward Wilfried Zaha, 26. ', 'Everton ilikuwa imewajumuisha wachezaji kama vile mshambuliaji wa Uturuki Cenk Tosun, 28, na kiungo wa kati wa Jamhuri ya Ireland James McCarthy, 28, katika ofa hiyo. (Mail)', 'Lakini Palace wanakaribia kufikia mkataba wa kumsajili McCarthy kutoka Everton kwa hadi £8.5m. (Sky Sports)', 'Everton wanakaribia kumsaini kwa mkopo beki wa Monaco Mfaransa Djibril Sidibe, 27. (Mail)', 'Vilabu hivyo vinafanya kila juhudi kuhakikisha Barcelona haimsajili tena mchezaji wao wa zamani. (Sport)', 'Lukaku kwa mara nyingine amefanya mazoezi na na wachezaji wa chini ya miaka 18 wa Anderlecht siku ya Jumanne, bila idhini ya United kuwa mjini Brussels. (Mail)', 'Mshambuliaji wa Manchester United raia wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, hajarejea kutoka Carrington kujiunga na mazoezi ya kikosi cha kwanza licha ya tetesi zinazohusiana na hatma yake ya baadae katika katika klabu hiyo. (Mirror)', 'Paris St-Germain imetoa ofa ya kumuuza mchezaji nyota wa Brazil Neymar, 27, kwa vilabu vya Manchester United, Juventus na Real Madrid.', 'Manchester United na Manchester City wametuma wataalamu wao kufuatilia mchezo wa kiungo wa kati wa Norway Hakon Evjen ,19 wakati wa mchuano wa Bodo/Glimt. (TV2 via Manchester Evening News)', 'Juventus wanajiandaa kuwapa Manchester United wachezaji watatu ili kubadilishana na kiungo Paul Pogba. (Mirror)', 'Mpango huo kama utafaulu, utawahusisha wachezaji Danilo, 28, na Joao Cancelo, 25. (Goal.com)', 'Arsenal wanaweza kuelekeza nguvu zao zote katika kumsajili beki wa kati wa RB Leipzig Mfaransa Dayot Upamecano, 20, kama mbadala wa beki wa Juventus Daniele Rugani - lakini Leipzig wanataka pauni milioni 50 ili kumuachia beki huyo. (Mirror)', 'Leicester haitamsajili Nathan Ake katika dirisha hili la usajili baada ya klabu ya Bournemouth kutaka dau la pauni milioni 75 kwa beki huyo raia wa Uholanzai. (Sky Sports)', 'Arsenal wamejaribu kufikia makubaliano na nahodha wao Laurent Koscielny - lakini beki huyo mwenye miaka 33, ambaye aligoma kusafiri na timu kwenda Marekani, pia amegoma kufanya mazungumzo na klabu. (Mirror)'] | 4 |
KATI ya wanawake watatu nchini, mmoja anaishi na aina fulani ya ugonjwa wa moyo, imefahamika.Takwimu hizo zilitolewa jana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), katika kambi maalumu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambacho kilele chake ni leo, ambako taasisi hiyo ilitoa huduma ya upimaji na elimu kwa wanawake waliojitokeza katika eneo la Soko la Kimataifa la Samaki, Feri jijini Dar es Salaam.Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Delila Kimambo alisema hata hivyo jinsi wanawake wanavyopata elimu juu ya ugonjwa huo, ndivyo wanavyoweza kujilinda katika jamii inayowazunguka. Dk Kimambo alisema magonjwa ya moyo na kiharusi husababisha vifo kwa mwanamke mmoja katika kila watatu wanaofariki, hii ni zaidi ya kujumlisha vifo vyote vinavyosababishwa na kansa.Aliongeza kwamba asilimia 90 ya wanawake wana kiashiria hatari kimoja au zaidi cha kupata magonjwa ya moyo na kwamba zaidi wanapata magonjwa hayo ni wale umri kuanzia miaka 20 na kueandelea. “Dalili za magonjwa ya moyo kwa wanawake haziko sawa na wanaume na mara nyingine dalili hatari huchelewa kutafsiriwa kwa haraka na watalaamu wa afya,” alisema.Alisema kwa bahati nzuri magonjwa ya moyo na kiharusi kwa asilimia 80 yanazuilika kwa kutoa elimu jinsi ya kujikinga na Kampeni ya Go For Women iliandaliwa na wanawake kwa lengo la kutoa elimu kwa wanawake duniani. Aidha, alisema wanawake wa JKCI wametenga siku ya jana kuelimisha wanawake wenzao na kutoa huduma ya upimaji kwani wanaamini elimu hiyo itasaidia jamii nzima.“Tupo hapa kuwatia moyo wanawake wote kutenga muda kidogo kutembelea wataalamu wa afya na kujua namba tano muhimu kwa afya ya moyo ambayo ni shinikizo la damu, jumla ya lehemu kwenye damu, kiasi cha lehemu nzuri ya kukinga na magonjwa ya moyo (HDL), kiasi cha sukari na uzito kulingana na urefu (BMI),” alieleza Dk Kimambo.Aidha, alisema tafiti zimeonesha kuwa uchaguzi wa mfumo bora wa maisha husababisha wanawake 330,000 kuepuka vifo vinavyotokana na magonjwa ya moyo kwa siku. Alisema wanawake wanapenda kutoa kipaumbele kwa wengine kuliko wenyewe hata hivyo wameshauriwa kujali afya zao pia ili wawe na fya bora watoe huduma kwao na jamii inayowahitaji. | 3 |
Na VERONICA ROMWALD-ALIYEKUWA KENYA WATU milioni saba hufariki dunia kila mwaka kutokana na matumizi ya bidhaa zitokanazo na tumbaku hususan uvutaji sigara, imeelezwa. Takwimu hizo ni matokeo ya utafiti wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wiki iliyopita Nairobi, Kenya katika warsha ya siku ya mbili ya kukabiliana na matumizi ya Tumbaku. Kwa mujibu wa WHO idadi ya wavutaji wa sigara huenda ikaongezeka hadi kufikia bilioni moja ifikapo 2025. WHO linaonya kuwa iwapo juhudi za kuelimisha jamii juu ya athari zitokanazo na bidhaa hizo hazitachukuliwa idadi ya vifo itaongezeka. Wadau wa sekta ya tumbaku walikutana hivi karibuni nchini Kenya kujadiliana namna ya kukabiliana na matumizi ya tumbaku kwa kutumia njia ya teknolojia. Katika warsha hiyo ya siku mbili iliyoandaliwa na Kampuni ya Oxygene, iliyopewa kauli mbiu isemayo ‘kupunguza madhara ya tumbaku, kuelekea dunia isiyo na wavutaji,’ waandishi wa habari zaidi ya 40 kutoka nchi mbalimbali barani Afrika walihudhuria. Nchi hizo ni pamoja na Tanzania, Kenya, Malawi, Zimbabwe, Uganda, Rwanda, Zambia, Botswana, Swaziland, Lesotho, Ethiopia, Nigeria, Mozambique na Afrika Kusini. Akiwasilisha mada katika warsha hiyo, Mshauri wa Vyombo vya Habari wa WHO, Magesha Ngwiri alisema takwimu zinaonyesha Bara la Afrika lina kiwango kikubwa cha wavutaji kuliko mabara mengine. “Linachangia kwa kiwango cha asilimia 80, matokeo ya utafiti wa WHO ya mwaka 2010/11 yanaonyesha vijana wenye umri kati ya miaka 13 na 15 barani humu walibainika wameanza kuvuta sigara,” alisema. Aliwataka waandishi kufanya utafiti wa kina kubainisha kiwango cha uvutaji kilichopo. “Lengo ni kuielimisha jamii na kuziamsha Serikali kuanza kuchukua hatua kukabiliana na hali hiyo,” alisema. Rais wa Shirika lisilo la kiserikali la Leadership Impact Dynamics, Ade Adeyami alisema iwapo hatua hazitachukuliwa itakuwa vigumu kwa Bara la Afrika kufanikisha lengo la tatu la Malengo Endelevu ya Dunia (SDGs). “Linahimiza afya bora kwa wote, takwimu zinaonyesha kiwango cha matumizi ya bidhaa zitokanazo na tumbaku duniani ni kikubwa kulinganisha na mabara mengine, lazima tuchukue hatua,” alisema. Mhadhili na mwanachama wa kudumu wa Taasisi ya Biashara ya Gordon, Chuo Kikuu cha Pretoria, Dk. Tendai Kadenhe Mhizha, alisema takwimu za Umoja wa Mataifa (UN) zilizotolewa mwaka 2012 zinaonyesha matumizi ya tumbaku yalisababisha vifo vya watu takriban milioni 38 duniani. | 3 |
KAMISHNA wa Bima, Dk Baghayo Saqware amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Wasimamizi wa Kampuni za Bima Afrika (AAISA) nafasi atakayoishika kwa kipindi cha miaka miwili.Saqware alichaguliwa hivi karibuni katika Mkutano Mkuu wa umoja huo ambao umemchagua Boubacar Bah ambaye ni Mkurugenzi wa Bima nchini Guinea, kuendelea kuwa Rais kwa kipindi cha miaka mingine miwili.Viongozi hao walichaguliwa na Mkutano Mkuu wa Pili uliofanyika juzi jijini Johannesburg, Afrika Kusini na kuhudhuriwa na wajumbe wake wote 24 kutoka nchi mbalimbali. Akizungumza na gazeti hili, Saqware alisema nafasi hiyo mpya itawezesha kufanya maboresho kwa sekta ya bima ambayo inaendelea kukua nchini na Afrika kwa ujumla.Alisema bima katika Afrika ina mambo mengi yanayofanana ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja kuyakabili. Mtafiti Mkuu kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima (TIRA), Dk Emmanuel Lupilya alimpongeza Saqware na kumtakia nguvu na mafanikio katika kipindi cha uongozi wake.Lupilya ambaye aliongozana na Saqware katika mkutano huo, alisema kama nchi, panahitaji ubunifu wa maendeleo, ujasiri katika uongozi na mipango ya kimkakati itakayoleta mabadiliko na ubora zaidi kwa sekta ya bima. Dk Saqware alisema ameweka vipaumbele vyake ambavyo pia vitanufaisha Tanzania ikiwemo kuendeleza na kuhakikisha sekta inafikiwa, inaaminika, inategemewa na kuwa kiunganishi.Katika mkutano huo, alishukuru wajumbe kumuamini na kumchagua kuwa Makamu Rais. Aliwahakikishia kuwa pamoja nao katika kuongoza umoja huo ambao Makao Makuu yake yako Yaoundé, Cameroon.Malengo makuu ya umoja huo ni kuendeleza ushirikiano miongoni mwa mamlaka za usimamizi kusaidia nchi zao katika suala zima la maendeleo ya raslimali watu. Mengine ni kutengeneza jukwaa kwa ajili ya kuwa na viwango sawa vya sheria ya bima na mfumo wa usimamizi katika bara.Ajenda kuu ya mkutano ilihusu kufahamisha wasimamizi kuhusu maazimio yaliyopitishwa Machi 31 na Aprili Mosi, mwaka huu Casablanca nchini Morocco; kupitisha Katiba na Sheria Ndogo za chama, Kutoa taarifa ya hali ya fedha, Kufanya uchaguzi wa Rais na Makamu Rais. Kwa mujibu wa Katiba ya chama, Mkutano Mkuu ni chombo kikuu cha uongozi | 3 |
Kisiga aliyewahi kutamba akiwa na klabu mbili za Simba na Mtibwa, ameamua kujiunga na timu hiyo iliyoshuka daraja baada ya kuahidiwa dau nono na uongozi wa timu hiyo.Akizungumza na gazeti hili msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, alisema wamemnasa mchezaji huyo lengo lao kubwa ni kukiimarisha kikosi chao na kuhakikisha wanarudi tena Ligi Kuu msimu wa 2016/17.“Tumekubali matokeo na tunachokifanya kwa sasa ni kukiimarisha kikosi chetu ili kuhakikisha tunafanya vizuri kwenye Ligi Daraja la Kwanza na kurudi tena Ligi Kuu ndiyo maana tumeanza na Kisiga,”alisema Bwire.Msemaji huyo alisema bado wanaendelea na zoezi la usajili kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara ambacho kinaweza kupambana kwa kucheza soka la kuvutia na kurudi tena kwenye ligi hiyo.“Tunajua kama Ligi daraja la kwanza ndiyo ngumu kuliko Ligi Kuu, ndiyo sababu tunapambana kuhakikisha tunaziba nafasi za wachezaji walioondoka ili tuweze kuwa imara kwa ajili ya kurejea tena Ligi Kuu."Msimu uliopita Kisiga alikuwa akiichezea klabu ya Simba, lakini mara kwa mara mchezaji huyo alikuwa kwenye malumbano na uongozi wa timu hiyo akituhumiwa kuihujumu timu pamoja na mkongwe Amri Kiemba na Haruna Chanongo, kitu kilichosababisha wenzake kutolewa kwa mkopo kwenye klabu za Azam FC na Stand United ya Shinyanga. | 4 |
Rais John Magufuli amesema kikokotoo cha mafao kilichokuwa kikitumika kwa kila mfuko wa jamii, kabla ya mifuko yote kuunganishwa kiendelee katika kipindi hiki cha mpito hadi mwaka 2023, ambapo wanachama 58,000 ndio watastaafu katika kipindi hicho.Amesema hayo katika mkutano wake na wawakilishi kutoka Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), vyama shiriki, watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PSSSF na NSSF pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii (SSRA) kuzungumzia kikokotoo cha mafao ya wastaafu."Katika kipindi hiki cha mpito, vikokotoo husika vitumike kwenye mifuko husika, ili kwamba mifuko ijiimarishe kwenye kipindi hiki na wastaafu pia wasipate shida katika kupata stahiki zao," aliongeza.Rais Magufuli pia ametoa maagizo kwa mifuko hiyo ya jamii kuboresha daftari la wastaafu, ili kuondoa wastaafu hewa na wanaotambulika zaidi ya mara moja.Vile vile amewaagiza kupunguza matumizi ya ovyo, na kuepuka kufanya uwekezaji usio na tija kwa kutumia fedha hizo za mafao ya wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji wa mifuko.Rais Magufuli ameeleza kuwa hadi kufikia mwezi Machi 2017, serikali ilikuwa imelipa deni lake lote la shilingi trilioni 1.2/- iliyokuwa ikidaiwa na mifuko ya jamii. | 3 |
Catherine Sungura – Mwanza HOSPITALI ya Rufaa ya Kanda Bugando (BMC), ipo mbioni kuanzisha taasisi ya moyo ili
kuweza kuhudumia wananchi wa kanda ya ziwa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa mwishoni
mwa wiki, Mkurugenzi wa hospitali hiyo Profesa Abel Makubi, alisema kuwa wapo mbioni kuanzisha taasisi
hiyo itakayokuwa na majengo mawili yenye ghorofa kumi na kumi na tano. Profesa Makubi alisema kuwa hadi kukamilika kwa majengo
hayo wanatarajia kutumia Sh bilioni 59 . “Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kwa dhati kutoa
huduma zote za kibingwa na bobezi hapa nchini,hii itapunguzia mzigo serikali na
wizara kupeleka wagonjwa nje ya nchi vilevile wananchi wa kanda hii kunufaika
na huduma za moyo huku huku,” alisema Kwa upande wa watumishi, Prof. Makubi alisema wameweza kuongeza
wataalam wa fani mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wakiwepo wauguzi, madaktari, madaktari
bingwa na bobezi na hivyo kufanya kazi ya utoaji huduma katika idara zote bila
kuteleleka. Hata hivyo aliishukuru Serikali kwa kusomesha
madaktari bingwa na bobezi kutoka
hospitali hiyo na hivyo kuifanya hospitali hiyo kutoa huduma za kibingwa
ikiwemo matatizo ya tumbo, mifupa, koo, pua na ndomo, macho, mfumo wa mkojo, meno,
ubongo na mishipa ya fahamu pamoja na matatizo ya akina mama. “Huduma za upasuaji kiujumla zimeboreka sana katika awamu
hii kwa upande wa upasuaji mkubwa wa
kawaida pia,upasuaji maalumu wa midomo sungura, kichwa maji na mgongo wazi
pamoja na upasuaji wa fistula,” alisema Prof. Makubi Aidha, aliishukuru Hospitali ya Taifa Muhimbili na
Taasisi ya Mifupa MOI kwa, ushirikiano wa karibu katika kutoa huduma za
kibingwa za upasuaji katika mikoa
mbalimbali ya Kanda ya Ziwa. | 3 |
NAIBU Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amesema anatamani tamasha la Utamaduni la Afrika Mashariki (JAMAFEST) liwe linafanyika kila mwaka kimzunguko kutokana na kuwepo kwa mambo mengi mazuri yanayowaunganisha. Mgalu alitembelea mabanda mbalimbali jana kwenye maonesho hayo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Sa- laam na kusema amefarijika kuona bidhaa nyingi, hasa zikiwa zinatengenezwa na kundi kubwa la akina Mama wa ukanda wa Afrika Mashariki.“Nimefarijika kuona baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na nishati, zinaweza ku- tumika kama nishati mbadala, nimeona tutashirikiana na wale ambao wako tayari, pia nimeona vitu vingi vizuri zaidi ya hivyo, kiasi kwambaushirikiano wa nchi hizo utaendelea katika kuhakikisha wanawauzia nishati ya umeme kwa siku zijazo kwa kuwa Tanzania ina uhakika wa kuzalisha umeme mwingi.“Mwito kwa nchi za Afrika Mashariki tujipange zaidi kwa mipango ya kiserikali ya kuweza kuwahakikishia wajasiriamali na wasanii wanatangaza Utamaduni wetu wa asili, niwapongeze wasanii na makundi mbalimbali kwa kutumia vyema fursa walizopata katika tamasha hilo, alisema. Alisema maonesho hayo makubwa yame- waweka pamoja na kushirikisha kila sekta hivyo, kuipongeza Wizara ya habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kufanikiwa kuandaa kwa kuwa wajasiriamali na wasanii wamekiri kuuza bidhaa zao. | 4 |
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amekerwa na mapato kidogo yanayotokana na uvuvi wa samaki katika bwawa la Mtera katika Wilaya ya Mpwapwa, mkoani Dodoma.Akizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo, Dk Mahenge amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri na Mkurugenzi wa Wilaya hiyo, Paulo Mwambasweya kuhakikisha wanapandisha mapato kwa kusimamia vizuri chanzo hicho pamoja na cha minada na mipakani.Pia amewataka viongozi hao, kuwaita na kuwahoji wahusika wote katika mnyororo mzima wa makusanyo ya mapato yatokanayo na samaki hadi yanapoingia katika mfuko wa halmashauri hiyo.Pia Dk Mahenge aliwataka viongozi hao kuunda tume ya madiwani ichunguze tena kuvuja kwa mapato ya halmashauri hiyo ambayo ni kidogo ukilinganisha na halmashauri ya Chamwino ambayo nayo inavua pia katika bwawa hilo.Dk Mahenge alisema inaonekana katika halmashauri hiyo kuna mchwa unaotafuna mapato yanayotokana na uvuvi wa samaki ni tofauti na halmashauri nyingine za Iringa Vijijini na Chamwino.Dk Mahenge alitoa mfano wa mapato ya Chamwino katika mwaka wa fedha wa 2018/19, ambapo kati Julai na Agosti Chamwino walikusanya Sh milioni 25, wakati Mpwapwa walikusanya Sh milioni 2.9 tu, kitendo ambacho alisema kinaonesha wazi bado kuna mianya ya upotevu wa mapato ya samaki.Alisema kutokana na upungufu wa mapato ya halmashauri, mkuu wa wilaya na mkurgenzi washirikiane na watendaji wa halmashauri wakiwa kama timu ili kila mmoja awajibike katika nafasi yake.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpwapwa, Donalt Ngwenzi akitoa neno la shukrani alisema, anashangaa kwamba katika siku nne walizoenda kusimamia mapato ya samaki walipata Sh milioni 7.9, lakini anashangaa halmashauri hiyo ndani ya miezi miwili ilikusanya Sh milioni 2.9 tu.Ngwenzi amesema, kitendo cha halmashauri hiyo kutopata mapato ya kutosha kutokana na uvuvi wa samaki katika Bwawa la Mtera ambayo ni madogo ukilinganisha na halmashauri nyingine, atalivalia njuga sana.Mkuu wa Wilaya, Shekimweri akizungumza baada ya maelekezo ya Mkuu wa Mkoa, alisema amesikia atafanyia kazi haraka kuwaita wahusika na kuwahoji nini kinasababisha mapato yao katika bwawa la Mtera yawe madogo ukilinganisha na Chamwino. | 3 |
Na JANETH MUSHI -ARUSHA
HAKIMU Mkazi, Desderi Kamugisha, amejitoa kuendelea kusikiliza moja ya kesi za uchochezi zinazomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema).
Katika kesi hizo, Lema anadaiwa kutoa matamshi yenye chuki na kuibua nia ovu kwa jamii.
Hakimu Kamugisha amejitoa katika kesi ya jinai namba 441/2016 ambayo Lema anadaiwa kutoa matamshi hayo Oktoba 23, mwaka jana wakati wa mkutano wa hadhara viwanja vya Shule ya Sekondari Baraa.
“Kiburi cha Rais kisipojirekebisha, Rais akiendelea kujiona yeye ni Mungu, mwaka 2020 haitafika Mungu atakuwa ameshamchukua maisha yake.
“Rais ana kiburi, Rais kila mahali watu wanaonewa, wafanyakazi wa Serikali hawana amani, wafanyabiashara hawana amani, watu wananyanyaswa,” Lema alinukuliwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Martenus Marandu.
Hakimu huyo sasa ataendelea kusikiliza kesi nyingine ya jinai namba 440/2016 ambayo pia inamhusu Lema anayedaiwa kutoa maneno ya uchochezi yenye kuleta tabaka miongoni mwa jamii Oktoba 22, mwaka jana maeneo ya Kambi ya Fisi, Kata ya Ngarenaro wakati wa mkutano wa hadhara.
Miongoni mwa maneno ambayo Lema anayodaiwa kuyatoa ni: “Rais Magufuli akiendelea na tabia ya kudhalilisha demokrasia na uongozi wa upinzani, iko siku taifa litaingia kwenye umwagaji wa damu.
“Rais yeyote ambaye haheshimu mipaka ya sheria, mipaka ya katiba, ataingiza taifa katika majanga na umwagaji damu, watu watajaa vifua, wakiamua kulipuka polisi hawa wala jeshi halitaweza kudhibiti uhalifu utakaojitokeza.”
Jana kesi hizo mbili zilipangwa kutajwa mbele ya Hakimu Kamugisha katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru, lakini Wakili wa Serikali, Alice Mtenga, alidai mahakamani hapo kuwa upelelezi umekamilika, hivyo wanaomba kupangiwa tarehe ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali.
Lakini Hakimu Kamugisha alisema haoni busara kuendelea kusikiliza kesi zote wakati kuna mahakimu wengine.
“Nilikuwa na kesi nne za mshtakiwa huyu huyu, sasa zimebaki mbili. Kwangu sioni kama itakuwa busara kusikiliza kesi zote wakati kuna mahakimu wengine wanaweza wakasikiliza, najiondoa kwenye kesi namba 441, nitaendelea na kesi moja namba 440.
“Ukiangalia nature ya kesi ni ile ile moja, mshtakiwa yule yule, kwa hiyo tutaenda kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi ili apangiwe hakimu mwingine wa kusikiliza kesi hiyo ili tarehe ya kusomwa maelezo ya awali itakayopangwa, asikilize hakimu mwingine,” alisema.
Katika kesi hizo, Lema anawakilishwa na Wakili Sheck Mfinanga.
Hata hivyo, mshitakiwa huyo hakuweza kufika mahakamani hapo jana kwa madai kuwa hawakuwa na taarifa za kesi hizo kupangwa.
“Nilikuwa nimesimama kwenye korido ya mahakama asubuhi nikamuona RCO, nikamuuliza kuna nini akanijibu amekuja kwenye hizi kesi, ndipo nikaamua kuja mahakamani ila Lema au wadhamini wake hawakufika,” alisema Mfinanga.
Lema alipandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Kamugisha Novemba 8, mwaka jana, akikabiliwa na kesi hizo.
Novemba 11, mwaka huo huo, alishindwa kupata dhamana baada ya mawakili wa Serikali kuwasilisha kwa njia ya mdomo kusudio la kukata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kupinga uamuzi wa dhamana uliotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.
Lema alikaa mahabusu ya Gereza Kuu la Kisongo kwa zaidi ya miezi minne kutokana na kukosa dhamana kuanzia Novemba 11 mwaka jana kabla ya kuachiwa kwa dhamana Machi 3, mwaka huu na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha. | 3 |
MAMLAKA ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA) kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wamezindua kanuni za kutoa huduma za bima kupitia benki.Akizindua kanuni hizo Jijini Dar es Salaam, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk Yamungu Kayandabila (pichani) alizitaka taasisi za fedha na benki nchini kuzingatia katika utoaji wa huduma ili kuongeza ufanisi wa shughuli zao. Alisema kanuni hizo zitasaidia kusambaza huduma ya bima nchini kwani watu wengi bado hawajafikiwa.“Ujio wa kanuni za kutoa huduma za bima kupitia benki nchini umechelewa kidogo, hivyo wadau wana kila sababu ya kuzingatia kwa manufaa ya pande zote watoa huduma na wanufaika,”alisema. Alisema endapo wadau watazizingatia kanuni hizo, mapato katika sekta hiyo kiujumla yataongezeka kwa taifa, watoa huduma na watu wengi zaidi watafikiwa na huduma za bima.Aidha, Kamishna wa TIRA, Dk Baghayo Saqware akizungumza katika hafla hiyo alisema licha ya manufaa lukuki ya uzinduzi wa kanuni hizo, pia unalenga kuendeleza ajenda ya TIRA ya kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za bima nchini yaani bima kwa wote.“Tunahitaji kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma za bima nchini kwa kuongeza aina za bima kwa mahitaji mbalimbali, mfano mbadala wa uuzaji na usambazaji wa huduma za bima ikiwemo kutumia benki,”alisema.Kamishna huyo aliongeza kuwa inahitajika teknolojia rahisi na rafiki kwa ajili ya kusambaza bima, kununua bima, kuuza bima, kulipa mafao, madai ya bima, kusikiliza maoni na mahitaji ya wananchi, kuchakata na kuandikisha maombi ya bima.Aliongeza kuwa kuanzishwa kwa kanuni hizo ni muhimu katika kuendeleza sekta ya kifedha nchini na kusisitiza kuwa pato la taifa, hasa ukizingatia faida nyingi ambazo zitapatikana kwa benki zenyewe na watumiaji wa huduma za bima. | 3 |
SERIKALI imezindua mfumo wa huduma ya uchunguzi binafsi wa ugonjwa wa Kifua Kikuuu (TB), matibabu na elimu kuhusu ugonjwa huo kupitia mitandao ya simu za mikononi ijulikanayo kama Tambua TB.Lengo kuu la afua hiyo ni kuongeza kiwango cha uibuaji wa wagonjwa wa TB na kuboresha upatikanaji wa huduma. Kwa kuanzia itatekelezwa kwenye mikoa sita ya Dar es Salaam, Pwani, Kilimanjaro, Arusha, Geita na Mwanza. Namna ya kuingia katika mfumo huo ni pamoja na kupiga namba *152*05# ambazo ni bure.Kwa mujibu wa ripoti ya TB ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) mwaka 2017, Tanzania ni miongoni mwa nchi 30 duniani zenye wagonwa wengi wa TB na takwimu za Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) za mwaka 2017, wagonjwa 69, 818 wa TB waligunduliwa ambao asilimia 90 walitibiwa na kupona.Hata hivyo, inakadiriwa kuwa wagonjwa wanaofikiwa ni asilimia 44, na kuna wagonjwa 84,000 wenye TB ambao bado wapo kwenye jamii na wanaendelea kuambukiza. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk F austine Ndugulile alizindua mfumo huo jijini Dar es Salaam jana na kuwaomba wadau wa maendeleo, wanaotekeleza shughuli za kifua kikuu nchini, kusaidia utekelezaji wa afua hiyo.Huduma hiyo imeandaliwa na wizara kwa kushirikiana na Shirika la PATH Tanzania/ KNCV-Challenge TB na Cardno- MHealth PPP Tanzania, ambapo wamefanikiwa kujumuisha ugonjwa huo kwenye teknolojia ya mtandao kwa kutengeneza mifumo miwili ya huduma ya uchunguzi binafsi wa TB na matibabu pamoja na elimu kuhusu TB.Dk Ndugulile alisema kupitia ujumbe wa uchunguzi binafsi, mtu yeyote anaweza kuingia na kujibu maswali kulingana na dalili za ugonjwa wa TB na baada ya kukamilisha, iwapo mteja ana dalili za TB, mfumo huo utamwelekeza kwenda kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu naye kwa uchunguzi zaidi na utaendelea kumkumbusha mpaka hapo atakapokubali kuwa amekwishatembelea kituo cha huduma za afya.Alisema kama matokeo yataonesha mteja hana dalili za TB, atashauriwa kujiunga na huduma ya ujumbe mfupi wa simu wenye kutoa elimu ya ugonjwa huo. Kuhusu upande wa huduma ya matibabu ya mgonjwa aliyethibitika kuwa na TB, Naibu Waziri alisema atasajiliwa kwenye mfumo na mtoa huduma wa afya pindi anapoanza matibabu. | 3 |
Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Pwani utafikishwa kwenye balozi za Tanzania nje ya nchi ili watu wa huko wazifahamu fursa zilizopo waje kuwekeza.Mkuu wa mkoa huo, mhandisi Evarist Ndikilo ameiagiza sekretarieti ya mkoa kuwasiliana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ili mwongozo huo ufikishwe kwenye balozi hizo.Jumamosi iliyopita Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliuzindua mwongozo huo wakati anafungua kongamano la uwekezaji Mkoa wa Pwani.“Leo tunaweza tukajivunia kwamba sasa tuna mwongozo wa uwekezaji katika mkoa wetu wa Pwani ambao umetokana na mawazo yetu sisi wenyewe, mawazo ya kila mtaalamu katika mkoa wetu wa Pwani. Leo tunaweza tukasema yeyote yule anayetaka kuja kuwekeza katika mkoa wetu wa Pwani afike kwa sababu tayari tuna mwongozo wa uwekezaji katika sekta zote”amesema Ndikilo mjini Kibaha.Ndikilo ameagiza mwongozo huo uwekwe kwenye tovuti ya mkoa huo, tovuti ya taifa na kwenye ukurasa wa mkoa kwenye mtandao wa kijamii wa instagram.“Kupitia teknolojia hii na utaalamu huu mwongozo wetu unaweza ukafika mbali kabisa kwa hiyo tujitahidi sana ili isiwe kwamba ni document (nyaraka) ambayo inaweza ikafichwa, iiishie katika makabrasha katika makabati hapana na mimi nilisema nataka kuona things are happening on the ground, tunataka kuona matokeo chanya kwenye jambo hili” amesema. | 5 |
NDEGE ya Shirika la Ndege la Ethiopia, Ethiopian Airlines aina ya Boeing 737 – 800MAX imeanguka leo saa mbili asubuhi wakati inatoka Addis Ababa kwenda Nairobi, Kenya.Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na ametoa pole kwa waliopoteza wapendwa wao.Kuna taarifa kwamba ndege hiyo iliyokuwa na mruko namba ET 302 ilikuwa na abiria 149 na wafanyakazi wanane.Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Ndege la Ethiopia, ndege hiyo yenye usajili namba ET- AVJ iliruka leo saa 2.38 kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa na ilitoweka kwenye mawasiliano saa 2.44 ikiwa kwenye eneo la Bishoftu.Taarifa hiyo inaeleza kuwa, kazi ya kuitafuta inaendelea na haijafahamika kama kuna waliosalimika au kupoteza maisha.Shirika hilo limesema, linaaminika kuwa ndege hiyo ilikuwa na abiria 149 na wafanyakazi wanane hivyo lipo kwenye mchakato wa kuthibitisha kwa kutumia taarifa za abiria za ndege hiyo.Mara ya mwisho ndege ya shirika hilo iliyokuwa ikitoka Beirut ilianguka Januari mwaka 2010 na kuua watu 90 wakiwemo abiria 83.Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema, wamesikitishwa na taarifa za ajali ya ndege dakika sita tu baada ya kuruka.Kwenye ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa twitter, Rais Kenyatta amesema, anaziombea familia za wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo.Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga ametuma salamu za rambirambi kwa watu wa Ethiopia na hasa familia na ndugu za waliokuwemo kwenye ndege hiyo. | 3 |
Na BADI MCHOMOLO TUPO mwishoni mwa mwaka, kama kawaida kwa wiki ya tatu sasa tunakuletea matukio muhimu yaliyopata kutingisha kwa mwaka huu. Leo tunakuletea listi ya mastaa wa mbele ambao walivalishana pete kwa lengo la kuoana, lakini ndoto zao hizo hazikukamilika hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu. Orodha hii ni hadi juzi Alhamisi wakati makala hii ikiandaliwa. Mariah Carey na James Packer Taarifa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii duniani zilienea habari za nyota wa muziki nchini Marekani, Mariah Carey kuvishwa pete ya uchumba na mpenzi wake, bilionea James Packer raia wa nchini Australia. Uhusiano wa wawili hao ulianza tangu 2015 mara baada ya Mariah kuachana na baba watoto wake Nick Cannon, ambaye alifanikiwa kupata naye watoto wawili mapacha, hivyo kuachana kwao kulimpa nafasi mfanyabiashara huyo kutoka nchini Australia kuonesha jeuri ya fedha. Hawakuchelewa kuonesha uhusiano wao, hivyo James aliamua kununua pete ya dhahabu yenye thamani ya zaidi ya bilioni 21 za Kitanzania, hapo hapo kutangaza ndoa ambayo waliweka wazi kuwa kabla ya mwaka 2016 kumalizika watakuwa wamefunga. Wengi walikuwa wanaisubiri ndoa hiyo kwa hamu kutokana na fedha zilizotumika kwenye kununua pete, lakini mambo yalikuwa tofauti siku chache baadaye, ambapo ndoto za wawili hao za kufunga ndoa mwaka huu zikafikia mwisho mwezi Oktoba. Kwa sasa wamebaki kuwa na mgogoro wa kupotezana muda. Blac Chyna na Rob Kardashian Blac Chyna ni mwanamitindo maarufu nchini Marekani ambaye alifanikiwa kupata mtoto wa kwanza akiwa na uhusiano na rapa Tyga, lakini Januari mwaka huu aliweka wazi kuwa anatoka na kaka wa Kim Kardashian, Rob Kardashian. Aprili mwaka huu, mrembo huyo alivishwa pete na mchumba huyo huku wakitangaza kutaka kufunga ndoa Desemba mwaka huu mara baada ya kufanikiwa kupata mtoto wao, kwanza walianza kwa kufanikiwa kupata mtoto mapema Novemba na ndipo watu wakawa wanasubiri ndoa ya wawili hao Desemba. Kwa sasa imebaki stori kwa kuwa wawili hao tayari wameachana mapema Desemba hii kwa madai kwamba familia ya Rob amekuwa na michepuko mingi, hataki ushauri kutoka kwa mrembo, pamoja na migogoro ambayo inaendelea ndani ya familia hiyo ya Kardashian, kwa sasa kila mmoja anaishi kivyake japokuwa wakiwa na mtoto wa mwezi mmoja. Nicki Minaj na Meek Mill Wawili hao wanafanya muziki wa Hip Hop nchini Marekani, walianza uhusiano wao tangu 2015, lakini mapema mwaka huu walitangaza kutaka kufunga ndoa mara baada ya Meek Mill kumvisha pete mchumba huyo. Mapema Novemba mwaka huu kulikuwa na taarifa kwamba wawili hao wameachana, lakini hakuna ukweli huo, bado wapo pamoja na wanaendelea na ratiba yao ya kutaka kufunga ndoa. Ukweli ni kwamba dalili za ndoa hiyo kufanyika mwaka huu hazipo japokuwa wapo kwenye uhusiano, hivyo kwa wiki hii moja iliyobaki kuingia 2017 ni asilimia chache wawili hao kufunga ndoa. Judith Nyambura ‘Avirl’ na Leslie Mugadza Judith Nyambura ni maarufu kwa jina la Avirl, ni nyota wa muziki kutoka nchini Kenya, tangu mwaka 2015 aliweka wazi kuwa anataka kufunga ndoa na mpenzi wake Leslie Mugadza kutoka nchini Afrika Kusini mara baada ya kumvisha pete. Juni mwaka huu, wawili hao walipanga kulimaliza jambo hilo lakini baada ya muda mrembo huyo aliweka wazi kwa mashabiki wake kwamba hakuna tena ndoa baada ya familia za pande zote mbili kushindwana katika mila, ndoa ya wawili hao ikabaki stori. Miley Cyrus na Liam Hemsworth Wawili hao ni wapenzi wa muda mrefu tangu 2012, na wamekuwa wakiachana na kurudiana ambapo ni zaidi ya mara mbili sasa, lakini Januari mwaka huu waliweka wazi kuwa wanataka kufunga ndoa lakini cha kushangaza hadi sasa dalili za kufunga ndoa hazipo kabisa wamebaki kuvishana pete. Jason Statham na Rosie Whiteley Hao ni nyota wa filamu, wamekuwa kwenye uhusiano wa wazi tangu 2010, lakini mapema mwaka huu Statham alifanikiwa kumvisha pete ya uchumba mrembo huyo ambapo hafla hiyo ilifanyika nchini Thailand, lakini hadi sasa kimya hakuna dalili zozote za ndoa yao. | 1 |
MSHAMBULIAJI wa Coastal Union, Ali Kiba amesema hakujiunga na timu yake mwanzoni kutokana kukabiliwa na majukumu mengine nje ya nchi ila sasa amerejea rasmi na yuko tayari kuitumikia baada ya kukosekana kwenye michezo mitatu ya mwanzo.Akizungumza juzi baada ya kushuhudia timu yake ikitoka sare ya 1-1 na KMC katika dimba la Mkwakwani Tanga alisema ameamua kuingia kwenye soka la ushindani na kusema anachotafuta ni tuzo upande wa soka kwani anaamini ana uwezo na tayari upande wa muziki ameshafanya vizuri"Lengo ni kufanikisha kupata medali au tuzo ya soka, najiamini nina kipaji cha kucheza mpira na kuimba, lakini sasa katika muziki tayari nimefanya mengi, nataka niwaoneshe watu kwamba ninaweza kufanya vizuri pia katika soka,” amesema Kiba.Alisema yeye na timu yake msimu huu wana lengo la kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.Kwa sasa Coastal Union inashika nafasi ya sita ikiwa na pointi tano baada ya kucheza michezo mitatu, ikishinda mmoja na kutoa sare mbili.Mbao FC inaongoza ligi ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Azam FC, Simba, Mtibwa Sugar na Stand United ila zikitofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa na idadi ya michezo. | 4 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.