text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
WAZIRI wa Maji, Profesa Makame Mbarawa ametishia kumweka ndani kwa siku tano Mhandisi wa Maji, Geofrey Oyao kutoka kampuni ya Orientation Construction Ltd anayetekeleza mradi wa maji kutoka mji wa Isaka na Kagongwa kwa kusuasua kukamilisha mradi huo na kutoa ahadi za uongo kuukamilisha.Ilidaiwa kuwa mradi ulipangwa kutekelezwa kwa kipindi cha miezi 18 kuanzia Julai 2017 hadi Desemba 2018 na kuongezewa tena muda hadi Juni 30,2019 lakini utekelezaji bado.Waziri Mbarawa alitoa kauli hiyo jana alipotembelea eneo la kijiji cha Kinaga kwenye utandazaji wa mabomba na kumueleza mhandisi huyo kuwa anampa mwezi mmoja ili ahakikishe amekamilisha kwa kuandikishana kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya kwa kujifunga mwenyewe.Alisema alitaka kumuweka ndani mhandisi kwa muda wa siku tano ili aweze kujifunza namna ya uharakishaji maana angetoka huko kazi ingeenda haraka kwani angekuwa amejifunza na kuongeza kuwa mkataba wanasainishwa na fedha nyingi wanachukua mradi hauendi.“Mkandarasi huyu mara kwa mara amekuwa akitoa ahadi za uongo kuhusu ukamilishaji wa mradi na wananchi wa maeneo ya Kagongwa na Isaka wanashida ya maji, nimetaka kumuweka ndani siku tano lakini nimeona nimpe fursa aende kwa Mkuu wa Wilaya wakaandikishane aahidi mwenyewe kwani mimi nataka ikifika mwezi Agosti mwaka huu awe amekamilisha,” alisema waziri Mbarawa.Waziri Mbarawa alisema jumla ya fedha za mradi huo ni kiasi cha Sh bilioni 22 na umekuwa na awamu mbili, awamu ya kwanza inahusu ujenzi wa bomba kuu la usafirishaji maji kwa gharama ya Sh bilion 10 na awamu ya pili inahusu ujenzi wa mfumo wa usambazaji maji katika miji midogo ya Isaka na Kagongwa.Mkurugenzi wa mamlaka ya usambazaji maji kwa miji ya Kahama na Shinyanga (Kashwasa) Joshua Mgeyekwa alisema kuwa mradi huu ulianza baada ya huduma ya maji iliyopo kutotosheleza mahitaji kwa miji ya Kagongwa na Isaka na umekuwa ukifanya kazi ya upanuzi wa mtandao wa maji wa Ziwa Victoria ikiwa mpaka sasa amefanikiwa kulaza urefu wa kilomita 49.54 kati ya kilomita 52.9 anazotakiwa kulaza.Mbunge wa jimbo la Msalala, Ezekiel Maige alisema mradi huo ulitakiwa kuanza mwaka 2017 na ukamilike mwaka 2018.
3
JULIET MORI NA LETICIA BWIRE (TUDARCO) MASHINDANO ya urembo ya Miss Tanzania yaliyofungiwa kwa muda wa miaka miwili yamepata ahueni baada ya Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kuipa kibali cha muda kampuni inayoendesha shindano hilo, International Agency Limited (LINO). Basata imetoa kibali hicho cha muda kisichozidi miezi minne kwa ajili ya maandalizi ya awali, ikiwemo kukamilisha usajili wa mawakala katika ngazi zote husika ili kuboresha na kurudisha heshima ya shindano la Miss Tanzania. Shindano la Miss Tanzania lilifungiwa Desemba 22 mwaka jana kwa muda wa miaka miwili na kuagiza kampuni hiyo kujipanga upya na kurekebisha kasoro zilizokuwa zikijitokeza mara kwa mara. Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa, Godfrey Mngereza, aliwaambia waandishi wa habari jana katika ukumbi wa baraza hilo uliopo Ilala, jijini Dar es Salaam kwamba kulikuwa na mapungufu ya mawakala wanaondesha shindano hilo. Alisema mawakala waliopo hawakufuata kanuni na taratibu za uendeshaji wa shindano hilo, ikiwemo mikataba ya washiriki na pia wengine hawakuwa na vibali vya kuendesha shughuli hiyo. “Tuna imani kwamba kampuni ya Lino itazingatia taratibu zote za uendeshaji wa matukio ya sanaa nchini na haitarudia makosa yatakayolisababishia shindano hilo kushuka viwango,’’ alisema.
1
Na MWANDISHI WETU – ARUSHA MWANASIASA mkongwe ambaye alipata kuwa mwenyekiti wa kundi la wabunge waliohitaji muundo wa Serikali tatu (G55) wakati wa utawala wa awamu ya pili, Njelu Kasaka, amesema hakuna mtu aliye salama ndani au nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kauli hiyo aliitoa wakati wa mkutano mkuu wa kidemokrasia uliofanyika jana jijini Arusha ambako alikuwa mgeni mwalikwa. Pasipo kutaja jina la mtu, Kasaka alitumia kauli hiyo kwa kugusia matukio ya kisiasa yaliyojiri katika siku za hivi karibuni. Moja ya matuko hayo ni lile lililotokea katikati ya wiki hii kwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kukabiliana na changamoto ya kutishiwa bastola na mtu anayeaminika kuwa askari kanzu.  “Ingekuwa wakati CCM ilipokuwa imeshika hatamu, suala hili la RC wa Dar es Salaam tayari CCM ingekuwa imeishakaa na kumuelekeza Rais cha kufanya juu ya mkuu huyo wa mkoa,” alisema Kasaka. Alisema siku hizi hali haiko hivyo ndiyo maana hata Katibu Mkuu wa CCM mwaka 2015 kabla ya uchaguzi mkuu, alitaka kodi kero zifutwe, lakini ndio kwanza zikaongezwa. “Ni kwa kuwa CCM ya sasa haina nguvu hizo tena, wapinzani wakiungana na kuondoa tofauti zao wanaweza kuiondoa CCM madarakani,” alisema. Kasaka ambaye amepata kuwa mbunge, waziri na mkuu wa mkoa, alijitoa ndani ya CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Mbali na Kasaka, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema wamiliki wa vyombo vya habari na waandishi wa habari hapa nchini sio maadui wa Rais Dk. John Magufuli bali adui yake ni yeye mwenyewe. Alimtaka Rais Magufuli badala ya kukasirikia vyombo vya habari ambavyo vinafanya kazi kubwa ya kuuhabarisha umma wa Watanzania, yeye binafsi ajitafakari na awe na akiba ya maneno pale anapozungumza. “Sijui kilichomkasirisha Rais ni kitu gani, mimi binafsi nashangaa, anasema kalamu za waandishi ndizo zitasababisha mauaji ya halaiki kama ilivyotokea katika nchi za jirani, sio kweli, badala ya kurudia rudia kutamka mauaji ya kimbari ya Rwanda, sisi tunamwambia aache na aweke akiba ya maneno. “Kama kiongozi wetu awe makini, awe mnyenyekevu na ajue hawezi kujua kila kitu, atuunganishe Watanzania, kwa sababu kile kilichotokea huko anakotolea kama somo ni matokeo ya utawala mbovu, ni itikadi ya jamii moja kujiona bora kuliko jamii zingine na ni matokeo ya wananchi kukosa matumaini,” alisema Zitto. Pia alitumia fursa hiyo kuendelea kulaani kitendo kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam cha kuvamia Clouds Media huku akiwa na askari. “Adui wa Rais Magufuli ni John Pombe Joseph Magufuli, ni kutokana na kuacha kutumia mifumo katika kutawala, matokeo yake viwanda havipanuki, ajira haziongezeki. Akirudi na kutumia mifumo atafanya vizuri. “Serikali haitakiwi kuhangaika na watu wadogo wadogo waliowekeza mitaji yao na kuajiri wafanyakazi, wala haitakiwi kuwafilisi, bali inapaswa kuangalia, kujadili na kuziba mianya yote ya ukwepaji kodi unaofanyika katika nchi yetu,” alisema. Akizungumzia dhana ya ujamaa, Zitto alisema tangu ujamaa ulipotupwa miaka 25 iliyopita pengo kati ya walionacho na wasio nacho limeongezeka na kiwango cha umasikini, hasa vijijini kinakua kwa kasi hali inayohatarisha umoja wa wananchi. Kwa mujibu wa Zitto, hali hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na sera mbovu za CCM na Serikali yake na hakiwezi kukwepa lawama na shutuma kwani ndio chama kinachotawala hivi sasa. Naye Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini,  Godbless Lema (Chadema), alisema kuwa amepata maono mapya, kwamba ameona viongozi mbalimbali wa dini; masheikh na maaskofu wakichomwa moto kutokana na kutenda dhambi ya woga. Lema alisema hayo wakati alipokuwa akitoa salamu za Chadema na kusisitiza umuhimu wa vyama vyote vya upinzani kuungana na kwenda kuwaelimisha wananchi madhara ya hofu na woga unaowakabili. “Nimepata maono, nimeona viongozi wa dini, mashekhe na maaskofu wakichomwa moto wa jehanamu, nikamuuliza Mungu kwanini, mbona hawa wanachomwa moto, akanijibu kwa sababu ya dhambi ya woga,” alisema Lema.
3
MTALII raia wa Ujerumani amekutwa amefariki dunia katika nyumba aliyokodi huko Kibweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja. Kamanda wa Polisi Mkoa wa mjini Magharibi Unguja, Awadh Juma Haji alithibitisha kufariki kwa Petern Lisches (43) aliyekuja mwaka huu.Mjerumani huyo alikodi nyumba ya kupumzika wageni inayomilikiwa na Jafar Hussein Kibweni mapema Januari mwaka huu akiwa ni mtalii. Aidha Kamanda alisema mwili wa marehemu uligundulika na mmiliki wa nyumba hiyo baada ya kutomwona siku moja na alipofuatilia katika chumba chake alikuta mwili umelala sakafuni.Kamanda alisema baada ya uchunguzi mwili wa mtalii huyo ulikutwa na kisu kidogo akiwa na majeraha sehemu ya mkono wa kushoto na sehemu ya shingoni na kutokwa damu nyingi. ‘’Uchunguzi wetu unaonesha mtalii huyo amejiua kwa kujijeruhi kwani hakuna harakati zinazoonesha kulikuwa na purukushani kumuua. Ametoka damu nyingi baada ya kujijeruhi mkono na mshipa mkubwa wa damu,’’alisema. Kamanda alisema uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo unaendelea na mawasiliano kuhusu mtalii huyo yanafanywa ubalozi wa Ujerumani nchini.
3
Muungano wa Vodacom na Cavalry Holdings Limited iliyokuwa na asilimia 17.2 ya hisa za Vodacom Tanzania, unahusu huduma za mawasiliano ya simu baada ya Tume hiyo kuridhia bila masharti maombi ya kampuni hizo.Kwa muungano huo, sasa Vodacom Group na Cavalry zitakuwa na jumla ya hisa 82.2, kwani awali, Vodacom Tanzania ilikuwa na hisa asilimia 65.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa FCC, Frank Mdimi, tume hiyo imeridhia maombi matatu ya muungano ya kampuni kwa mujibu wa kanuni Namba 42(13) ya Kanuni za Utendaji za Tume ya Ushindani za mwaka 2013.Alisema tume hiyo imeridhia maombi matatu ya muungano wa kampuni hizo katika kikao chake cha 55 cha mashauri ya ushindani kilichofanyika Aprili 17, 2014 baada ya maombi hayo kuwasilishwa katika Ofisi za Tume kati ya Desemba 20, 2013 na Machi 28, 2014 na kampuni zilizokuwa zikikusudia kutekeleza makubaliano ya muungano huo.Mdimi alitaja muungano mwingine ulioridhiwa na tume hiyo ni baina ya kampuni za AVIS Southern Africa na Tanzuk Limited ambao muungano wao unahusisha biashara ya ukodishaji wa magari pamoja na huduma zinazoambatana nazo na muungano baina ya kampuni za Dutch Oak Tree Foundation na Tanga Dairies Co-operative Union na Tanga Fresh Limited ambazo muungano wao unahusisha sekta ya biashara ya maziwa.
5
DAKTARI bingwa wa magonjwa ya macho katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dk Frank Sandi amewasihi wananchi kukinga macho yao pindi wanapofanya shughuli ambazo zinaweza kusababisha majeraha kwenye macho.Akizungumza kwenye kambi maalumu ya macho, Sandi alisema majeraha kwenye macho ni moja ya matatizo ambayo wameyabaini wakati wa kufanya uchunguzi wa awali. “Tumewakuta ambao macho yao yana majeraha na hii inatokana na mtu kutokinga macho anapofanya shughuli zake, hivyo niwasihi sana wananchi kuhakikisha wanalinda macho yao,” alisema.Alisema katika kambi hiyo ambayo itafikia tamati yake Ijumaa, asilimia 30 ya watu waliofanyiwa uchunguzi wamekutwa na matatizo ya mtoto wa jicho, huku wengine wakikutwa na matatizo ya uoni hafifu, vikope na majeraha kwenye jicho. Dk Sandi alisema katika siku mbili za kambi wamewafanyia upasuaji wagonjwa 150 huku wale waliotibiwa matatizo ya macho ni 250.“Tumepanga kuwafanyia uchunguzi wagonjwa 1,500 na kuwafanya upasuaji wagonjwa 400, huduma hizi kwa wagonjwa ambao tumewatoa vijijini matibabu yanatolewa bure, na wanaofika hospitali wenyewe hulipia Sh 2,000 tu isipokuwa kwa wale walio na kadi za bima ya afya,” alisema.Naye Matha Tuguti mwenye umri wa miaka 110, alisema anashukuru kwa huduma alizopata bure kwani alikuwa haoni kabisa na sasa anaona baada ya kufanyiwa upasuaji. Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), na Chuo cha Utah nchini Marekani wameandaa kambi maalumu ya matibabu ya macho kwa lengo la kuwafikia wananchi ambao hawafikiwi na huduma za macho kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Dodoma.
3
Ushindi huo unaifanya Simba izidi kujikita kileleni kwa kujikusanyia pointi 41 juu ya Azam na mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 34 na Azam yenye pointi 33. Iliichukua Simba dakika 37 kuandika bao pekee katika mechi hiyo ambayo vinara hao wa ligi walitawala zaidi kipindi cha kwanza.Okwi alifunga bao hilo baada ya kuunganisha krosi safi ya Asante Kwasi kabla ya kuujaza mpira wavuni. Kabla ya kufunga bao hilo, Okwi ‘Mhenga’ alipata nafasi kadhaa za kufunga katika dakika ya 5, 24 na 28 ambapo zote ama zilidakwa na kipa wa Azam Razak Abalora au zilitoka nje.Azam ilionekana kubadilika katika kipindi cha pili ambapo benchi lake la ufundi lilianza kwa kufanya mabadiliko kwa kumtoa Mbaraka Yusuf na kumuingiza Shaaban Iddi. Mabadiliko hayo yaliifanya timu hiyo kubadilika kwani sasa mashambulizi yalifika langoni mwa Simba na dakika ya 49 Yahaya Zaud alipata nafasi lakini alipiga mpira pembeni.Aidha katika mechi hiyo kulikuwa na ubabe wa hapa na pale ikiwa ni pamoja na mfungaji wa bao la Simba Okwi kufanyiwa madhambi ya mara kwa mara na mabeki wa Azam. Pengine hiyo ndio sababu ya benchi la ufundi la Simba kumtoa nyota huyo wa Uganda katika dakika ya 84 na nafasi yake kuchukuliwa na Nicholas Gyan.Katika mechi nyingine za ligi zilizochezwa jana, Mwadui imeutumia vema uwanja wake wa nyumbani kwa kuichapa Mtibwa Sugar mabao 3-1 huku Mbao ikishindwa kufanya hivyo kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1.Simba: Aishi Manula, Shomary Kapombe, Erasto Nyoni, Yussuph Mlipili, Asante Kwasi, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Said Ndemla/ Muzamil Yassin dk59, John Bocco, Emmanuel Okwi/ Nicholaus Gyan dk84, James Kotei.Azam FC:Razak Abalora, Daniel Amoah, Bruce Kangwa, Yakubu Mohammed, Aggrey Morris, Stephan Kingue, Iddi Kipagwile/ Salum Abubakar dk55, Frank Domayo, Mbaraka Yussuph, Yahya Zayed/Bernard Arthur dk71,Enock Atta-Agyei
4
NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM TIMU ya Simba imeanza kuipigia hesabu Mbeya City wanayotarajia kucheza nayo Oktoba 17 mwaka huu kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya, wekundu hao wamedai kuwa ili kuzoa pointi zote tatu wamepanga kufika mapema mkoani humo. Wachezaji wa Simba ambao hawamo kwenye timu za Taifa, wanatarajia kuanza tena mazoezi leo baada ya mapumziko ya siku mbili, tayari kabisa kujiandaa na mchezo huo muhimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Msimu uliopita Simba iliambulia patupu mbele ya Mbeya City, baada ya kufungwa mechi zote mbili walizocheza na timu hiyo, ilianza kufungwa mabao 2-1 Uwanja wa Taifa kabla ya kulala 2-0 mkoani Mbeya. Akizungumza na MTANZANIA jana, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Haji Manara, alisema wataondoka jijini hapa mapema kuelekea Mbeya ili kuzoea mazingira ya huko na kutimiza lengo lao la kulipa kisasi. “Tunahitaji ushindi kwenye mchezo na Mbeya City hivyo tutahakikisha tunaupata na tumejipanga kwenda mapema kabisa mkoani humo na kujiandaa kikamilifu kuchukua pointi tatu,” alisema. Manara alisema kwa upande wa wachezaji, wote wapo katika hali nzuri kimchezo na wataanza kufanya mazoezi yao katika Uwanja wa Boko Veterani jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ratiba ya ligi, Simba ilitakiwa kucheza na Ndanda katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona wikiendi iliyopita, lakini mchezo huo umepigwa kalenda ili kupisha maandalizi ya mchezo wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ dhidi ya Malawi ‘The Flames’ utakaofanyika keshokutwa. Simba hivi sasa inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo ikiwa na jumla ya pointi 12, baada ya kucheza mechi tano, wakishinda nne African Sports (1-0), Mgambo Shooting (2-0), Kagera Sugar (3-1), Stand United (1-0) huku ikifungwa 2-0 na Yanga.  
4
RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amesema matumizi ya vitambulisho vipya vya kielektroniki vya Mzanzibari Mkaazi yataiwezesha serikali kuweka na kuhifadhi kumbukumbu za matukio ya watu wote katika Daftari la Usajili na Utambuzi.Dk Shein alisema hayo katika uzinduzi wa kadi mpya za kielektroniki za Mzanzibari mkaazi, hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Shehe Idrisa Abdul Wakil Kikwajuni mjini hapa.Alisema matumizi ya vitambulisho hivyo yataisaida serikali, taasisi na watu binafsi kupanga vipaumbele vya utekelezaji wa shughuli mbalimbali zenye nasaba na huduma za maendeleo ya kijamii.Aidha, alisema kuwepo kwa mfumo huo wa matumizi ya vitambulisho vipya utaisadia serikali kuwatambuwa watu wanaostahiki kupata haki za msingi kama ilivyobainishwa katika Katiba ya Zanzibar ya 1984.“Itawezesha kumtambua mtu anayestahili kupata haki yake kama malipo ya pensheni, haki za matibabu, kujiunga na masomo,” alisema Dk Shein na kuongeza kwa vitambulisho hivyo serikali itapata urahisi kukusanya mapato na kuimarisha huduma muhimu za kijamii, afya, elimu, barabara na ulinzi na usalama wa raia na mali zao.Alisema serikali inapaswa kuwa na nyenzo kudhibiti amani na utulivu wa watu wake, hivyo ni dhahiri vitambulisho vipya vitakavyotumika hivi sasa ni vyenye ubora wa hali ya juu na uwezo wa kuhifadhi taarifa nyingi za mtumiaji.Alieleza kuwa vitambulisho hivyo vimetengenezwa kwa teknolojia ambayo sio rahisi kughushiwa, vikiwa na uwezo mkubwa wa kiusalama wa taarifa za mtumiaji, akibainisha kutumika katika nchi kadhaa duniani.Alitoa mwito kwa wakazi wote wa Zanzibar wa miaka 18 kwenda kujisajili katika ofisi za Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii zilizopo katika wilaya zote nchini, sambamba na wale ambao hawajajiandikisha kufanya hivyo.Aidha, aliwataka watendaji wanaohusika na utayarishaji vitambulisho hivyo, kuwa makini katika utoaji wake.Vile vile aliwataka wakuu wa mikoa kusimamia vizuri taarifa za uhakiki wa watu walioko katika maeneo yao, kuanzia ngazi za shehiya, wadi na wilaya ili kuhakikisha wanawatambua wananchi wao na taarifa zao zilizo sahihi.“Ni muhimu mlifanyie mapitio daftari la wakaazi katika shehiya, ambalo ndio msingi wa uthibitisho wa kujua taarifa za utambuzi na makazi ya watu waliomo katika maeneo yenu,” alisema.Alisisitiza haja ya kulinda na kudumisha amani na utulivu uliopo nchini, akibainisha kuwa bila ya kuwepo amani na utulivu nchini, hakutakuwa na maendeleo yoyote yatakayofikiwa
3
HISTORIA ya Tanzania imesheheni matukio yanayoifanya iwe kati ya nchi zilizokuwa na ushawishi mkubwa kimataifa tangu uhuru ukilinganisha na nafasi yake kiuchumi na hata kijiografia.Ukweli huu ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliyeuambia ulimwengu baada ya uhuru kwamba uhuru wa wetu hautakuwa na maana kama nchi nyingine katika bara letu zitakuwa bado zinatawaliwa.Tamko hilo liliiweka nchi yetu katika nafasi imara ya kidiplomasia, kwani lilikuwa nguzo muhimu ya kuimarisha uhusiano na mataifa mengine ya kikanda na kimataifa. Wapinga ukoloni wote na waliokuwa katika harakati za kudai uhuru, walijikuta wakiwa wadau katika wazo hilo la Mwalimu Nyerere.Siyo hilo tu bali na mengine mengi kama vile Tanzania ilivyouambia Umoja wa Mataifa kuwa Jamhuri ya Watu wa China ilistahili kuwamo, hali iliyolifanya taifa kubwa kama China kuvutiwa na kunufaika na ushawishi wa Tanzania kwa mataifa mengine. Lakini pia watu wa mataifa mengine walivutiwa na jinsi Mwalimu Nyerere alivyoijenga Tanzania katika misingi ya umoja na amani, Watanzania wote wakiwa wamoja bila kujali tofauti za itikadi zao za kisiasa, kikabila na kidini.Aidha, misingi hii imeijengea heshima Tanzania mpaka ikaitwa “kisiwa cha amani” huku ikiwa mstari wa mbele katika kulaani ubabe, uonevu na ukandamizaji popote pale ulipotokea duniani bila kuogopa.Pamoja na mambo mengine, Tanzania, ikiwa imejizatiti katika misingi ya kidiplomasia, kwa nyakati tofauti ilijitolea katika ukombozi wa nchi zilizokuwa chini ya tawala za kikoloni, hasa zile za kusini mwa bara la Afrika. Kielelezo kizuri cha mchango wa Tanzania katika jumuiya ya kimataifa ni nishani ya heshima ya juu aliyopewa Dk Salim Ahmed Salim na nchi ya China kwa kutambua mchango wake katika kuitetea ili irudishiwe kiti chake Umoja wa Mataifa katika miaka ya 1970.Aidha, mchango wa Dk Salim katika kuimarisha uhusiano kati ya China na Tanzania wakati aliposhikilia nyadhifa mbalimbali ulitajwa kama sababu ya kutunukiwa nishani hiyo. Vilevile, mchango wa Dk Salim katika kujenga uhusiano mzuri kati ya China na Afrika, akiwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), umetajwa pia kuwa sababu nyingine ya kutunukiwa nishani.Chini ya uongozi wa Rais John Magufuli, Tanzania imeendelea kuwa mshirika mzuri katika jumuiya mbalimbali za kimataifa, katika Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, Jumuiya ya SADC na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kupitia ushiriki wake Tanzania imeendeleza misingi ya Baba wa Taifa ya kupinga dhuluma, kuhimiza maendeleo barani Afrika, kulinda amani, umoja na mshikamano. Kwa sasa, Tanzania ikiwa ndiye mwenyekiti wa SADC, inaendelea kutumia diplomasia katika kukuza uhusiano na ustawi katika nchi wanachama wa SADC, kwa kuitaka jumuiya ya kimataifa kuiondolea nchi ya Zimbabwe vikwazo vya kiuchumi.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi alipokuwa akifungua kongamano la kumbukizi ya Mwalimu Nyerere hivi karibuni, alisema Tanzania haiko katika dunia yake yenyewe na kwamba, katika kujiletea maendeleo, huona fahari katika kushirikiana na nchi nyingine.“Ni msimamo wetu kuwa nchi za SADC haziwezi kujiletea maendeleo katika nchi wanachama kama wenzetu wanakabiliwa na vikwazo. Nimefurahi kusikia kuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mko katika maandalizi ya kongamano ambalo, pamoja na mambo mengine, litajadili mustakabali wa vikwazo kwa maendeleo ya Zimbabwe na Afrika kwa ujumla,” alisema.Sera ya mambo ya nje pia inaitaka Tanzania kuimarisha utendaji wa mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali ambayo yanafanya kazi nchini ili kuhakikisha huduma mbalimbali zinazotolewa na mashirika hayo zinaendana na sheria za nchi, ambapo kwa Tanzania pia tumeshuhudia asasi mbalimbali zikifanya kazi zake hapa nchini.Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekabidhiwa usimamizi na mapitio ya sera, ambapo pamoja na mambo mengine, imepewa jukumu la kuratibu shughuli zote kimataifa na kuimarisha shughuli zote kidiplomasia zinazoiunganisha Tanzania na mataifa mengine duniani. Ili kufanikisha malengo hayo, Tanzania inatumia mikakati mbalimbali ili kuendana na mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi, kwa kuzingatia misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa letu.Mikakati hiyo imejikita katika kutengeneza mazingira mazuri ya ndani na nje ya utekelezaji wa sera hiyo ili kuimarisha diplomasia. Malengo ya sera hiyo ni pamoja na kuanzisha, kuhimiza na kulinda maslahi ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiuchumi ya Tanzania kupitia diplomasia endelevu ya kiuchumi. Malengo mengine ya sera pia ni kuhakikisha mahusiano ya Tanzania na nchi nyingine au mashirika ya kimataifa yanachochewa ili kukuza maslahi mapana ya kiuchumi.Kujenga uchumi wa kujitegemea, kuimarisha amani na usalama wa taifa na kusaidia juhudi za kikanda na kimataifa ili dunia iwe na amani ni malengo mengine ya sera hiyo. Ukuaji wa uchumi wa kidiplomasia Moja kati ya mambo yanayotiliwa mkazo na serikali ni kuimarisha na kukuza uhusiano wa kimataifa pamoja na diplomasia ya uchumi, ambapo mabalozi wa nchi yetu wamekuwa tegemeo kubwa katika kuhamasisha malengo hayo.Diplomasia ya uchumi ni dhana pana lakini kwa lugha nyepesi ni uwakilishi wa nchi nje ya nchi na mara nyingi hujikita katika mambo ya kiuchumi, ambayo ni pamoja na kuvutia wawekezaji, kuvuta watalii na kuhamasisha fursa za biashara. Kupitia wawakilishi wetu katika muktadha huo wa kukuza diplomasia ya uchumi Mwezi Aprili 2019, Serikali ilipokea watalii 1,000 kutoka Israel.Aidha, mwezi Mei, 2019 serikali pia ilipokea watalii 330 wakiwemo wafanyabiashara na wawekezaji kutoka China. Watalii hao walikuwa ni kundi la kwanza miongoni mwa watalii 10,000 ambao wanatarajiwa kutembelea Tanzania mwaka huu. Mazao 10 ya Tanzania yapata soko China Katika mkutano wa 15 wa kimataifa baina ya China na nchi jirani na nchi marafiki, uliofanyika mwaka 2018 nchini humo, mazao 10 kutoka Tanzania yalipata wanunuzi katika masoko ya China.Mazao yanayohitajiwa kwa wingi katika soko la China ni korosho, kahawa, mbaazi, choroko, dengu, chai, tangawizi, asali na muhogo. Sekta ya Elimu Katika kuhakikisha kuwa uhusiano kati ya China na Tanzania unazidi kukua katika sekta ya elimu, pamoja na kuimarisha ushirikiano wa miaka 55, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kilisaini makubaliano ya ushirikiano na chuo kikuu cha Beijing katika masuala ya sheria.Makubaliano hayo yalifanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Juni 2019 wakati wa uzinduzi wa kituo cha mafunzo ya sheria kwa nchi za Afrika. Haya yote yanaonesha namna diplomasia yetu ya uchumi inavyoimarika katika taifa hilo linaloibuka kwa ukubwa duniani hususani katika miaka hii minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya tano.
3
MKOA wa Pwani umeidhinishiwa Sh bilioni 240.3 na Bunge kutekeleza mpango wa maendeleo, zikiwa ni bajeti ya sekretarieti ya mkoa na mamlaka za serikali za mitaa kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020.Hayo yalisemwa mjini Kibaha mkoa wa Pwani juzi na Katibu Tawala Msaidizi, Mipango na Uratibu, Edward Mwakipesile wakati wa kikao cha ushauri cha mkoa (RCC). Mwakipesile alisema kuwa bajeti kubwa iko kwenye mishahara ya watumishi ambapo mkoa utatumia Sh bilioni 154.9 huku zile za miradi ya maendeleo zikiwa ni Sh bilioni 51.9“Fedha za matumizi mengineyo itakuwa ni kiasi cha Sh bilioni 33.4 huku fedha za ndani zikiwa ni Sh bilioni 39.3 na fedha za nje zitakuwa ni Sh bilioni 12.6,” alisema Mwakipesile.Alisema changamoto za utekelezaji mpango wa bajeti ni kuchelewa kwa fedha za miradi ya maendeleo.“Uchakavu wa vitendea kazi, kompyuta, printa, mashine za kudurufu na magari husababisha ufanisi wa kazi kupungua, upungufu wa wafanyakazi, makatibu muhtasi na wahudumu wa ofisi,” alisema.Aidha alisema suluhu ni kuwasiliana na Wizara ya Fedha na Mipango ili fedha zitolewe kwa wakati.Alisema suluhisho ni kuomba kuajiri watumishi kulingana na mahitaji na sekretarieti ya mkoa inatarajiwa kutoa Sh bilioni 60.4 hadi Septemba na Halmashauri ya mji na wilaya zimekusanya Sh bilioni 33.6.
3
RAMADHAN HASSAN-DODOMA WAZIRI wa Madini, Dotto Biteko, amesoma bajeti ya wizara yake kwa mara ya kwanza tangu apandishwe kutoka naibu waziri na kuwa waziri kamili, ambapo amesema sheria mpya ya madini, ukuta wa Mererani, umeleta mapinduzi katika sekta hiyo. Akisoma bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2019/20 bungeni jijini hapa jana, alisema kutokana na sheria ya madini na mikakati ya kudhibiti utoroshwaji wa bidhaa hiyo, Serikali imetaifisha madini ya Dola za Marekani milioni 13.5 na Sh milioni 6.3 Alisema kwa Tanzanite, mwaka 2018, wachimbaji wadogo pekee wamechangia Sh bilioni 1.4 na uzalishaji umeongezeka kutoka kilo 147.7 hadi 781.204. Biteko alisema Tume ya Madini kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, vimekuwa vikiendelea kudhibiti utoroshwaji madini kuhakikisha rasiliamali hiyo inatumika kwa manufaa ya Watanzania. Alisema hadi kufikia Februari, zilikamatwa karati 66.60 za madini ya almasi yenye thamani ya Dola za Marekani 34,782.52  jijini Dodoma. “Aidha, gramu 77.0 za madini ya dhahabu zenye thamani ya Sh milioni 6.3 zilikamatwa mkoani Tabora na kilo 75,957.30 za madini ya vito yenye thamani ya Dola za Marekani 1,795,87.87 zilikamatwa jijini Dar es Salaam,” alisema Biteko. Alisema kilo 5.72 za madini ya dhahabu yenye thamani ya Sh milioni 389.7 zilikamatwa mkoani Geita, gramu 11,445.52 za madini ghafi na karati 1,351 za vito vyenye thamani ya Sh milioni 206.5 zilikamatwa mkoani Arusha huku tani 3.7 za madini ya Rhodelite, zenye thamani ya Dola za Marekani  50,162.46 zilikamatwa mkoani Morogoro. Biteko alisema mkoani Mwanza yalikamatwa madini ya dhahabu kilo 319.594 yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 11.7. MADINI YATAIFISHWA Alisema madini yaliyokamatwa katika Mikoa ya Dodoma, Tabora, Mwanza na Dar es Salaam yalitaifishwa. Aidha alisema madini yaliyokamatwa mikoa ya Arusha, Morogoro na Geita yapo katika hatua mbalimbali ya uchunguzi. “Mpaka Machi, madini ambayo yaliyotaifishwa yalikuwa na thamani ya Dola za Kimarekani milioni 13.5 na Sh milioni 6.3,” alisema Biteko. MAOFISA MADINI WAKAZI WAIMARISHA ULINZI Biteko alisema ulinzi umeimarishwa katika maeneo yote ya uzalishaji kwenye migodi mikubwa na ya kati kwa kuwaweka maofisa madini wakazi (MROs). Alisema lengo la kuweka maofisa hao ni kusimamia na kuwasilisha taarifa za uzalishaji wa kila siku pamoja na kudhibiti mianya ya utoroshwaji madini. Katika maeneo ya viwanja vya ndege na mipakani, alisema wamewekwa wasimamizi kuhakikisha madini yanayopitishwa yana vibali husika na kuzuia utoroshaji. “Nitoe wito kwa Watanzania kufanya shughuli za madini kwa kuzingatia sheria za nchi ikiwemo Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 kama ilivyorekebishwa mwaka 2017 pamoja na kanuni zake,” alisema. ONYO KWA WATUMISHI Biteko alibainisha kuibuka kwa matukio ya baadhi ya watumishi wasio waaminifu kushirikiana na wachimbaji na wafanyabiashara madini wasio waaminifu kuiibia Serikali mapato kupitia kuwasilisha taarifa zisizo sahihi za uzalishaji madini. “Katika kuhakikisha tunakomesha tabia hii isiyo ya kizalendo inayopelekea Serikali kupoteza mapato, Serikali imeendelea kuchukua hatua kali za kinidhamu ikiwemo kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi na kuwafikisha mahakamani waliobainika kuwa na makosa,” alisema. WACHIMBAJI WADOGO WAONGEZA MAPATO Kuhusu uendelezaji wa eneo la kimkakati kwenye migodi ya Mirerani, Biteko alisema baada ya kujengwa ukuta kuzunguka mgodi huo, udhibiti madini ya Tanzanite umeimarika na hivyo kuongeza ukusanyaji maduhuli yatokanayo na madini hayo. Alisema wachimbaji wadogo wameitika wito wa kulipa kodi ambapo sasa wanalipa kuliko kipindi chochote kwenye historia ya uchimbaji kwenye eneo hilo. “Wachimbaji wadogo Mirerani walikuwa wanachangia kwa asilimia 6 hadi 10 ya mapato yote, kiasi kikubwa kilikuwa kikichangiwa na mgodi wa TanzaniteOne.  “Mwaka 2017 Sh bilioni moja zilikusanywa, kati ya fedha hizo Sh milioni 930 zilikusanywa kutoka mgodi huo kama mrabaha wa ada ya ukaguzi ikiwa sawa na asilimia 85 ya mapato yatokanayo na uzalishaji wa Tanzanite na Sh milioni 164.1 sawa na asilimia 15 zilikusanywa kutoka kwa wachimbaji wadogo,” alisema. Alisema mwaka 2018, wachimbaji wadogo pekee wamechangia Sh bilioni 1.4 na uzalishaji umeongezeka kutoka kilo 147.7 hadi 781.204. Biteko alisema ili kutekeleza majukumu ya wizara hiyo katika mwaka wa fedha 2019/20, aliliomba Bunge kuidhinisha na kupitisha makadirio ya sh bilioni 49.4 kwa matumizi ya kawaida na maendeleo. UPINZANI Akiwasilisha jana bungeni, msemaji mkuu wa upinzani katika Wizara ya Madini, John Heche, alisema katika mwaka huu wa fedha, wizara hiyo iliidhinishiwa Sh bilioni 19.62 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Alisema hadi kufikia Februari, wizara hiyo ilikuwa imepokea Sh milioni 100, sawa na asilimia 0.5 ya bajeti iliyoidhinishwa. MAONI YA KAMATI Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mariam Ditopile, alisema licha ya Serikali kudhibiti utoroshwaji wa madini, kamati inashauri kuendelea kuwekwa mikakati endelevu na mbinu za kisasa kudhibiti biashara ya madidi isiyo rasmi. MAONI YA WABUNGE Mbunge wa Viti Maalumu, Neema Mgaya (CCM) alisema ukuta wa Mererani mkoani Arusha umeweza kuokoa madini ambayo yalikuwa yakitoroshwa nje ya nchi. Mbunge wa Nyang’wale, Hussein Amar (CCM), aliitaka Serikali ichukue hatua za haraka kuhakikisha wachimbaji wadogo wanapata leseni. Maftaha Nachuma (CUF) wa Mtwara Mjini, alihoji kuhusiana na utekelezaji wa mlundikano wa leseni zaidi ya 99  za uchimbaji wa madini ya Tanzanite katika eneo la Mirerani.   Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma (CCM) alidai kwamba kuna shida kubwa kwa watendaji katika wizara hiyo kutotimiza wajibu wao, hivyo alitaka wanajeshi waende wakafanye kazi. BAJETI YAPITA Akihitimisha mjadala wa wizara yake, Biteko alisema kipaumbele cha awamu ya tano ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata haki yake. “Urasimu, Serikali itachukua hatua kuhakikisha wananchi wanapata haki zao. “One Stop Centre tunataka kuwaondolea urasimu na hilo litakuwa jengo moja katika ofisi moja,” alisema. Kuhusu wafayakazi wa wizara yake kutokuwa waaminifu, Biteko  alisema jambo hilo analichukua na watalifanyia kazi. “GGM wameanza kulipa fidia, kama kuna mwananchi anadhani hajalipwa vizuri awasiliane na wizara yangu, kuna mtu amelipwa milioni 74 mara ya kwanza, lakini pia ameleta jina mara ya pili anataka alipwe tena, sio sawa Mheshimiwa Spika, lazima tuwalinde wawekezaji,” alisema.
3
WASHINGTON, Marekani OFISA wa ngazi ya juu wa intelijensia nchini hapa amesema   huenda Urusi inakiuka mkataba wa nyuklia kwa kufanya majaribio ya silaha zisizo na nguvu kubwa katika ene la Actic. Akizugumza   mjini hapa jana, Luteni Jenerali Robert Ashley ambaye ni  mkurugenzi wa taasisi ya intelijensia  amesema serikali ya Urusi pengine inakiuka  sheria za mkataba wa  pamoja wa   CTBT unaozuia majaribio ya nyuklia ambao Urusi ilitia saini mwaka 2008  na ambao Marekani imetia saini lakini haijaanza kuutekeleza.  ”Kwa uelewa wetu uendelezwaji wa silaha za nyuklia unatusababisha tuamini kuwa shughuli za majaribio ya Urusi zitasaidia kuboresha uwezo wa silaha za nyukilia,” alisema Luteni Jenerali Ashley. Ameongeza kuwa Marekani ilitegemea Urusi, ambayo amesema ilikuwa inategemewa kujaribu silaha zake katika visiwa vya Zemlya  kuongeza ubora wa silaha za nyuklia kwa   muongo mmoja ujao. Hata hivyo  wachambuzi wa mambo wamepokea taarifa hiyo lakini haikuwashawishi.  Shirika linalosimamia utekelezaji wa makubaliano ya mkataba wa nyukilia CTBTO, limesema kwenye taarifa yake kuwa haishuku shughuli zozote zinazokwenda kinyume na mkataba. CTBT unapiga marufuku majaribio ya silaha za nyukilia popote  duniani  uliofikiwa kwenye mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 1996.   
2
Arodia Peter, Dodoma Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, ameitaka Serikali kufuatilia na kutoa taarifa za kutekwa kwa kijana na kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mdude Nyagawa ambaye anadaiwa kutekwa. Mdude anadaiwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana kwenye ofisi yake Mbozi, mkoani Songwe juzi, Mei 4 wakiwa na silaha za moto. Chenge ametoa maelekezo hayo bungeni jijini Dodoma leo Jumatatu Mei 6, wakati akijibu hoja ya Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa aliyetoa hoja ya kuahirisha Bunge kwa kutumia kanuni ya 64 kuhusu kujadili jambo la dharura. Katika hoja yake, Msigwa alisema hivi karibuni kumekuwapo na matukio ya watu kutekwa, kupotea na hata kuuawa, huku akitolea mfano madai ya kutekwa kwa kada wa chama hicho, Mdude. Akitoa maelezo ya hoja hiyo, Chenge ameitaka Serikali kutolea ufafanuzi jambo hilo. “Ni kweli suala lolote linalohusu uhai wa binadamu, itakuwa vizuri Serikali itoe maelezo ili wananchi wajue hali ilivyo,” amesema Chenge. Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusufu Masauni amesema Jeshi la Polisi limeanza kufanyia uchunguzi tangu jana, Mei 5, na wameongeza nguvu kutoka makao makuu ya jeshi hilo. Aidha Masauni ameomba wananchi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola kuhusu utata wa tukio hilo.
3
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama, Nkone ni mwimbaji wa kwanza wa Tanzania kukubali kushiriki katika tamasha hilo la Amani linalotarajia kufanyika Oktoba 4, mwaka huu jijini Dar es Salaam na katika mikoa 10 mingine nchini.“Upendo Nkone amekubali kushiriki katika tamasha letu hili la kuombea amani wakati wa Uchaguzi Mkuu. Kamati ya Maandalizi inamshukuru sana mwimbaji huyu kwa kuthamini amani ya nchi,” alisema Msama.Msama alisema wanaendelea na mchakato wa kuzungumza na waimbaji wengine ili kuwa na idadi kubwa ya waimbaji wa Tanzania sambamba na wengine kutoka nje.Alisema wanajipanga kualika waimbaji kutoka nchi tano za Afrika kwa lengo la kunogesha uzinduzi huo ili ujumbe wa neno la Mungu ufike kwa dhati.Aidha, Msama alisema sambamba na waimbaji kutoka nje ya Tanzania pia wanajipanga kutangaza amani katika mikoa 10 ya Tanzania Bara.“Tunaendelea na mikakati ya kufanikisha Tamasha hilo ambalo litakuwa ni la aina yake, hivyo wadau mbalimbali wasubiri tamasha hilo,” alisema Msama.Msama alisema tamasha hilo litahudhuriwa na wadau mbalimbali kwa kushirikisha wanasiasa, viongozi wa dini mbalimbali na makundi mengine kama wasanii na wanamichezo.
4
JERUSALEM, Israel MAMLAKA za dola nchini hapa zimesema   zina ushahidi wa kutosha unaoonyesha Waziri Mkuu, Benjamin Netanyahu anahusika na vitendo vya rushwa na ufisadi ingawa yeye anakanusha akidai tuhuma hizo zinasambazwa na wapinzani wake wa siasa. Polisi hao walisema jana kwamba  uchunguzi wao unaonyesha  Waziri Mkuu  Netanyahu alipokea rushwa   kuingilia kati  katika moja ya kesi ambazo zilikuwa zikiikabili kampuni kubwa ya mawasiliano ya Bezeq. Polisi walisema   wana ushahidi huo ambao unaonyesha wazi    Netanyahu  na mkewe Sara, walipokea rushwa hiyo na kufuja fedha  hizo  kupindisha ukweli. Katika madai hayo Netanyahu anashuhutumiwa kujichotea mamlioni ya dola katika kampuni hiyo ya  Bezeq  kuviziba mdomo vyombo vya habari vilivyokuwa vikiripoti kesi hiyo. Washauri wake wawili waandamizi wamegeuka kuwa mashahidi  na wanasema wamezipa mamlaka ushahidi wa kutosha unaothibitisha kuwapo  vitendo hivyo. Waandishi wa habari ambao hapo awali walifanya kazi katika tovuti ya Walla wamewahakikishia polisi kuwa walisumbuliwa  na kulazimishwa kuandika habari nzuri tu zinazomuhusu Netanyahu. Hata hivyo Netanyahu anakanusha taarifa hizo akisema zilianza kusambaa hata uchunguzi bado haujaanza kufanyika. Kutokana na taarifa hiyo ya polisi kumeibuka wito wa kumtaka  Netanyahu ajiuzulu. “Waziri Mkuu hana tena sifa ya kuendelea kushikilia nafasi yake ni lazima ajiuzulu hata leo,” alisema  Tamar Zandberg, ambaye anaongoza Chama chenye mlengo wa kushoto cha Meretz. “Israel ni lazima iingie katika uchaguzi,”aliongeza kiongozi huyo. Hiyo ni mara ya tatu kwa polisi  kutangaza mashitaka dhidi wa waziri mkuu  huku mkewe akiwa ameshashitakiwa katika kesi tofauti zinazohusiana na matumizi mabaya ya fedha za serikali.
2
Azam FC haikuwa na kazi nyepesi kwani katika dakika zote 90 timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1 na kuongezewa muda wa dakika 30 na kushindwa kutambia baada ya kutoka sare ya 2-2 kabla ya kupigiana penalti.Shujaa wa Azam FC alikuwa beki Aggrey Morris, aliyefunga penalti ya tano na kuamsha shangwe kwa wachezaji wenzake. Wengine waliofunga penalti za Azam FC ni John Bocco, Himid Mao, Allan Wanga na Waziri Salum wakati zile za Mwadui zilifungwa na Malika Ndeule, Iddi Moby na Jabir Aziz.Aliyekosa upande wa Mwadui ni Kevin Sabato. Dakika 90 za mchezo huo zilimalizika timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1, Azam FC ikitangulia kwa bao la Khamis Mcha ‘Vialli’ dakika ya tatu kabla ya Mwadui kusawazisha kupitia kwa dakika ya 82.Katika dakika 30 za nyongeza Azam walitangulia tena kwa bao la Mcha dakika ya 97, kabla ya Jabir Aziz kuisawazishia Mwadui dakika 120. Kwa upande wa Coastal Union na Yanga katika mchezo mwingine wa nusu fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani, mchezo huo ulivunjika katika dakika ya 110.Kwa mujibu wa taarifa kutoka Tanga, ilidaiwa kuwa mchezo huo ulivunjika wakati Yanga ikiwa mbele kwa mabao 2-1 uwanjani hapo kufuatia mshika kibendera namba mbili kupasuliwa juu ya jicho la kushoto kwa jiwe lililotupwa na shabiki. Coastal Union ilitangulia kwa bao la kiungo Mcameroon, Youssouf Sabo kabla ya Yanga kusawazisha kupitia kwa mshambuliaji Donald Ngoma, ambapo mabao yote yalifungwa kipindi cha pili.Amissi Tambwe akaifungia Yanga bao la pili mwanzoni tu mwa dakika 30 za nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1. Msemaji wa Coastal Union, Oscar Asenga mwenyewe alidaiwa kuwa timu yao ilionewa na mwamuzi, ambao walikuwa wakiipendelea wazi Yanga.Kwa upande wa Azam FC wenyewe walipata bao katika dakika ya tano lililowekwa kimiani na Khamisi Mcha dhidi ya wenyeji Mwadui ya Shinyanga katika mchezo huo wa nusu fainali ya Kombe la FA.Mcha aliifungia tena Azam FC bao la pili katika dakika ya saba ya muda wa nyongeza na kuifanya timu hiyo kuwa mbele kwa mabao 2-1. Jabir Azizi alifunga kwa penalti katika dakika ya 14 kipindi cha pili cha muda wa nyongeza na kufanya matokeo kuwa 2-2 hadi zinamalizika dakika 120 za mchezo huo.Bado haijajulikana mchezo huo wa Yanga na Coastal Union kama utarudiwa au Yanga watapewa ushindi. Coastal Union walitawala zaidi dakika ya 55 hadi 58 hasa katikati ya uwanja, huku Yanga walionekana wakichanganyikiwa na kupoteza mipira mingi bila sababu.Hatimaye Coastal walifanikiwa kupata bao la kuongoza katika dakika ya 54 mfungaji akiwa ni Yossiuf Sabo kwa shuti kali la chini baada ya kazi nzuri ya Ayoub Semtawa kuwachambua mabeki wawili wa Yanga.Donald Ngoma aliisawazishia Yanga bao katika dakika ya 60 baada ya mabeki wa Coastal Union kusimama wakifikiri kuwa mchezaji huyo Mzimbabwe alikuwa ameotea. Hadi dakika 90 za mchezo zinamalizika kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1 na kuongezewa dakika 30.
4
Aidha alisisitiza wafanyabiashara kuhakikisha kuwa sukari inaendelea kusambazwa na kuuzwa kwa wananchi bila kuihodhi. Awali, juzi alipozungumza na waandishi wa habari, Simwanza alisema bei elekezi ya sukari ilikuwa Sh 2,000 kwa Dar es Salaam na miji jirani.Kwa upande wa mikoa iliyo pembezoni, bei ilielekezwa iwe 2,200. Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema juzi wakati akisisitiza bei elekezi hiyo (ya awali), kulikuwa na kikao kingine kikiendelea kujadili suala la sukari, ambacho ndicho kilifikia uamuzi wa bei ya Sh 1,800 baada ya kujiridhisha.“Kuhodhi bidhaa ni kuhujumu uchumi wa nchi, sukari ni bidhaa nyeti inayohitajika sana. Tunawataka wafanyabiashara wote watii agizo hili,” alisema Simwanza. Alisema maofisa wa bodi ya sukari Tanzania, kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za serikali, hususani maofisa biashara wa mikoa na wilaya watafuatilia na kusimamia utekelezaji wa agizo hilo la bei elekezi.“Serikali ikisema kitu ni amri. Niseme tu hatutasita kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wale watakaobainika kupandisha bei au kuhodhi bidhaa hiyo,” alisema Simwanza. Juzi Simwanza akizungumza na vyombo vya habari alisema upatikanaji wa sukari nchini ni wa kuridhisha na ipo akiba ya kutosheleza nchi nzima.Alisema pamoja na baadhi ya viwanda kusimamisha uzalishaji wa sukari kutokana na msimu kuisha, hali ya bidhaa hiyo nchini ni nzuri na ipo zaidi ya tani 62,000. Aliwataka wasambazaji wakubwa wa sukari hususani kampuni ya Alneen Enterprise ya jijii Dar es Salaam , ambayo imethibitisha kuwa na sukari tani 8,600, waitoe na kuiuza.Wakati huo huo, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji, Charles Mwijage alisisitiza kuwa hakuna uhaba wa sukari nchini na kuwataka wafanyabiashara walio na leseni za kuingiza na kuuza bidhaa hiyo, kutoificha.Mwijage alitaka watu wenye taarifa juu ya mfanyabiashara aliyefungia sukari katika ghala lake ampelekee, afunge ghala husika mara moja. Alisema serikali inajikita zaidi katika uanzishaji wa viwanda vya sukari na kuongeza ajira na si katika kuagiza sukari kutoka nje.Miongoni mwa jitihada hizo ni pamoja na mazungumzo inayofanya na mwekezaji anayetaka kuwekeza katika ujenzi wa kiwanda cha sukari mkoani Kigoma, atakayewasili nchini wakati wowote kukamilisha taratibu.
5
Rais John Magufuli amewakaribisha wananchi wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) waje kununua bidhaa zinazozalishwa nchini ikiwemo saruji, sukari, mafuta, bidhaa za chuma, na vyakula yakiwemo mahindi.Rais Magufuli pia amewakaribisha wananchi wa DRC waje kuwekeza kwenye sekta ya viwanda, kilimo, uvuvi, utalii, madini nk.Amewakaribisha wananchi wa DRC kuja kuuza madini kwenye masoko ya madini nchini.'Kwa hiyo kila kitu, tunakaribishana na sisi wote ni ndugu, na kwamba, watu wa DRC waione Tanzania kama nchi yao, na Watanzania waione DRC kama nchi yao" amesema Rais Magufuli Ikulu, Dar es Salaam.Amesema Tanzania na DRC zimekubaliana kuondoa vikwazo vya biashara na uwekezaji ili wananchi katika nchi hizo watumie fursa zilizopo."Na katika kufanikisha hilo tumekubaliana kuzihimiza taasisi zetu za kifedha hususani benki kufungua matawi kwenye nchi zetu mbili ili kuwarahishia wananchi kupata huduma za kibiashara..."Hii ni opportunity (fursa) nyingine kwa wakuu wa mabenki mbalimbali. Nakumbuka CRDB wamefungua matawi mpaka Burundi, sasa ni wakati wa kufungua matawi mpaka DRC ili kusudi kufacilitate (kuwezesha) biashara itakayokuwa inafanyika kati ya wananchi wa nchi hizi mbili"amesema Rais Magufuli.Amesema, Tanzania imeamua kuongeza muda wa kutunza mizigo ya DRC katika bandari ya Dar es Salaam kutoka siku 24 hadi 30, imeondoa katazo la ufunguaji makontena na imefuta tozo ya kusindikiza mizigo inayokwenda nchini humo.Amesema, Tanzania na DRC zimekubaliana kubadilishana uzoefu wa kutumia rasilimali ili ziwanufaishe wananchi katika nchi hizo.Rais Magufuli pia amesema, Rais wa DRC, Felix Tshisekedi amekubali Tanzania ipeleke walimu wa Kiswahili nchini humo wakafundishe kwenye vyuo vikuu.
5
Baada ya juzi wanariadha watatu kutwaa medali kwenye michezo hiyo inayofanyika Los Angeles, jana wanariadha watano waliibuka na medali.Akizungumza kwa njia ya mtandao jana, Mkuu wa msafara, Frank Macha alisema Tanzania imeendelea kujinyakulia medali baada ya juzi kupata medali tatu.“Wachezaji wetu wamefanikiwa kupata medali nyingine tano baada ya zile tatu ambazo zilinyakuliwa awali."Waliopata medali ni Blandina Patrick (dhahabu) na Deonatus Manyama (fedha) wote kwenye mbio za mita 800. Wengine ni Faraja Meza aliyepata medali ya dhahabu, Riziki Chilumba medali ya fedha na Aisha Kaoneka medali ya shaba kwenye mbio za mita 100.Wachezaji wengine ambao walishajinyakulia medali ni Godfrey Jabuya, Blandina Patrick na Deonatus Manyama kwenye mbio za mita 400 hivyo hadi sasa Tanzania imefikisha jumla ya medali nane, dhahabu tatu, fedha tatu na shaba mbili.Timu hiyo ina wachezaji wanane, wanawake wanne na wanaume wanne, itashiriki tena katika mchezo wa riadha katika mita 100, 200, 400, 800, 5000, nusu marathon na mita 4x100 kupokezana vijiti
4
Na MWANDISHI  MAALUM -HAVANA WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba hapa nchini, Lucas Polledo, ambapo amewakaribisha wafanyabiashara wa nchi hiyo kuja kuwekeza nchini katika viwanda vya dawa. Alisema kwa sasa Serikali ya Tanzania inaagiza dawa kutoka nje ya nchi jambo ambalo linasababisha kutumia fedha nyingi, hivyo uwepo wa kiwanda utasaidia kupunguza gharama. Pia wawekezaji watakuwa na uhakika wa soko la bidhaa zao. Waziri Mkuu aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Balozi Polledo mjini Havana. Majaliwa yuko Cuba kwa ajili ya ziara ya kikazi yenye lengo la kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Alisema Serikali imedhamiria kuendeleza sekta ya viwanda nchini kama mkakati wa kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati, hivyo wafanyabiashara kutoka nchini Cuba wanakaribishwa kuja kuwekeza nchini, hususani katika viwanda vya dawa na sukari. Waziri Mkuu alisema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu wa kisiasa, pia imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji, jambo ambalo litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini. Pia alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Cuba kwa ushirikiano mzuri na Serikali ya Tanzania kwa sababu Cuba ni mojawapo kati ya nchi zenye ushirikano wa muda mrefu na Tanzania. “Tanzania na Cuba zina historia ya kutosha. Tunatambua mahusiano mazuri yaliyopo kati nchi zote mbili, ambayo yalikuwepo kuanzia Serikali ya awamu ya kwanza chini ya uongozi wa Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Nyerere,” alisema Majaliwa. Kwa upande wake, Balozi Polledo alisema Serikali ya Cuba itahakikisha uhusiano wake na Serikali ya Tanzania unaendelea kuimarishwa. Pia alipongeza jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuboresha maendeleo pamoja na kukuza uchumi.
3
Na JOHANES RESPICHIUS-DAR ES SALAAM MWANAZUONI maarufu barani Afrika, Profesa Patrick Lumumba, amesema Rais Dk. John Magufuli na Rais wa Rwanda, Paul Kagame si madikteta bali wanachokifanya ni kuhakikisha kunakuwa na siasa za miiko na maadili. Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam jana katika Mkutano wa Pan African Humanitarian wa mwaka huu ulioandaliwa na Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa (Yuna) uliokuwa na kaulimbiu ya “amani inawezekana jana, sasa na kesho” na kuwakutanisha vijana kujadili nafasi zao katika kuleta amani barani Afrika. Profesa Lumumba ambaye ni raia wa Kenya, alisema katika miaka ya hivi karibuni, wamekuja viongozi wenye mwelekeo na uchungu wa kuhakikisha mataifa yao yanaendelea, lakini baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiwaita madikteta. “Tunapaswa kujua hawa watu tunaowaita madikteta ni akina nani, kwa sababu kuna viongozi wameibuka katika miaka mitatu hadi 20 iliyopita, wakiwa na mwelekeo na kuona uchungu wa kuhakikisha mataifa yao yanaendelea, lakini baadhi ya watu wengine wanawaita eti ni madikteta,” alisema na kuongeza: “Lakini viongozi hao ni watu wazalendo na wakereketwa wa maendeleo endelevu, hivyo watu kama hawa lazima tujiulize mienendo yao ni ya kidikteta? Au ni ya kuhakikisha mataifa yao yanapiga hatua za haja na hoja. Mfano wengine wanasema Kagame, Dk. Magufuli ni dikteta, sikubaliani nao kwa sababu kile ambacho wanakifanya, wanajaribu kusema kwamba lazima kuwe na siasa za miiko na maadili. “Nakubali kwamba udikteta ni jambo ambalo halistahili, lakini ni muhimu kuhoji kwamba uhuni ndiyo demokrasia? Kwa sababu kumeibuka wimbi la watu ambao ni wababaishaji hata sio wapinzani, kila kitu anachokifanya (rais) wao kazi yao ni kupinga.” Akizungumzia suala la amani, hasa katika vipindi vya uchaguzi, alisema ni wakati wa kujiuliza ni aina gani ya uongozi inahitajika barani Afrika ili kuwe na njia ya kubadilisha uongozi isiyoleta vurugu tofauti na ilivyo sasa. “Pia tunapaswa kuangalia hivi vitu tunavyoviita vyama, ni vyama kweli au ni vikundi tu, genge tu la vibarua waliokuja kujitafutia nyadhifa ili kupora mali za Waafrika. Vijana ndio wataibua hoja hii na kutathimini kuwa mataifa yetu tunayaandaa kwa minajili ya kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo,” alisema. Pia alisema anaamini Afrika itakuja kuwa na amani na utulivu kwa sababu jitihada mahsusi zimeshaanza kufanywa na viongozi wake na tayari wamekwisha kutoa tamko kwamba kufikia mwaka 2020, lazima vitu vinavyoleta migogoro vitolewe na kila mtu anatakiwa kushiriki kwa nafasi yake.
3
MKUU wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga, akimkabidhi panga, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime na Rorya, Andrew Satta, kwa ajili ya kuendelea na oparesheni ya kufyeka mashamba 37 ya bangi wilayani humo. Picha na Shomari Binda NA SHOMARI BINDA, UONGOZI wa Wilaya ya Tarime umefyeka mashamba 37 ya bangi  yenye ukubwa wa ekari 56 wilayani humo katika oparesheni ya siku mbili, imeelezwa. Oparesheni hiyo iliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya, Andrew Satta  na vikosi vya mbalimbali  ulinzi na usalama. Vilevile, walikamata magunia 20 ya bangi kavu yenye uzito wa tani moja ambayo yalikuwa yamekwisha kuandaliwa na kutunzwa kwa ajili ya kupelekwa sokoni. Kamanda   Satta, alisema katika oparesheni hiyo walikamatwa watuhumiwa 14 ambao wanajishughulisha na kilimo cha bangi. Alisema watu hao  wanaendelea kuhojiwa na upelelezi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani. DC Luoga   akizungumzia katika Kijiji cha Nyarwana na Matongo Kata ya Kibasuka, alisema katika oparesheni zote ambazo zimekuwa zikifanyika  hiyo imefanikiwa zaidi. Alisema kuharibiwa  mashamba na kukamatwa magunia hayo ya bangi kumetokana pia na ushirikiano kutoka kwa wananchi wa maeneo hayo. Luoga alisema mikakati kabambe inaendelea kuandaliwa  kukomesha kilimo cha bangi ikiwamo kuanzisha kilimo cha miwa katika mabonde. "Tulianza mapema kupambana na zao haramu la bangi na maagizo kutoka ngazi ya taifa itaendelea kutusukuma  katika mapambano haya na naamini tutafanikiwa na hizi oparesheni tunazoendelea nazo zinatusidia. "Kuna watu ambao   wanakuwa kama wanakwamisha jitihada hiuzi sasa hatuwezi kukubaliana nao na tutawashughulikia," alisema Luoga. Alisema muda umefika kwa wale wanaojihusisha na kilimo cha bangi kujisalimisha na kuachana na zao hilo haramu .
3
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), imezindua muongozo wa huduma za tiba za dharura, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi nje ya hospitali.Mwongozo huo unaelekeza jamii pembezoni mwa barabara kuu kutoa taarifa ya ajali, wataalamu kufanyia kazi taarifa za ajali na wataalamu na madereva kusafirisha majeruhi eneo la tukio hadi hospitali.Uzinduzi wake umefanyika jana es Salaam wakati wa kufunga mafunzo ya watoa huduma za tiba ya dharura, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi wa ajali na wagonjwa wa dharura kutoka nje ya hospitali. Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Dharura na Maafa wizarani, Dk Elias Kwesi alisema mradi wa majaribio utaanza Oktoba mwaka huu ukishirikisha vituo vya afya na hospitali zilizopo pembezoni mwa barabara ya Dar es Salaam hadi Mbeya kwa lengo la kuokoa maisha ya majeruhi pindi wanapopata ajali.Dk Kwesi alisema tafiti zinaonesha kuwa asilimia kubwa ya majeruhi hufa wakati wanapokimbizwa hospitalini kutokana na kutokuwepo kwa utaalamu wa namna ya kuwabeba wagonjwa hao vizuri. Alisema ajali zinapotokea hakuna magari ya wagonjwa yaliyokuwa yakifuata majeruhi na endapo yakifuata majeruhi, hakuna wataalamu wa kusaidia majeruhi hivyo, wakati mwingine husababisha vifo.“Katika mwongozo huu tutawaelewesha namna ya kubeba majeruhi kwa sababu wapo waliopata ulemavu kutokana na kubebwa vibaya pindi wanapopata ajali. Lakini kushirikisha magari ya wagonjwa yaliyopo katika vituo vya afya vya karibu ya eneo la tukio ili kuokoa majeruhi wote,” alisema Dk Kwesi. Alisema pia gharama za mradi huo ni Sh bilioni 11 na Sh bilioni 7.5 zimetengwa kwa ununuzi wa magari ya kubebea wagonjwa, ukarabati wa vituo vya afya kutoa huduma za dharura, mafunzo na uandaaji wa mifumo ya kompyuta.Alifafanua kuwa gharama za uendeshaji wa mradi huo ni Sh bilioni 2.5 na baada ya matokeo chanya watafanya mazungumzo na Benki ya Dunia ili kuanza kwa mradi huo nchi nzima. Mkuu wa Mafunzo ya huduma za tiba ya dharura MUHAS, Dk Henry Sawe alisema wizara iliwapa dhamana ya kuandaa na kuendesha mafunzo huduma za dharura kwa wataalamu 225.Dk Sawe alisema walivuka lengo hilo na kutoa mafunzo kwa wataalamu 519 katika makundi ya wataalamu wa wagonjwa nje ya hospitali, wasaidizi wa wataalamu, wataalamu wa kupokea simu za dharura, watoa huduma ngazi za jamii na wakufunzi wa watoa huduma. Alisema serikali iliwataka kutoa mafunzo kwa wataalamu wa wagonjwa wa nje ya hospitali 45 na vituo vya afya na hospitali saba ikiwemo Kimara, Muhimbili, Tumbi, Chalinze, Ruaha Mbuyuni, Mtakatifu Kizito Mikumi na Hospitali ya Rufaa Morogoro.Dkt Sawe alisema mafunzo hayo yalianza Novemba 13, mwaka jana na yalijumuisha wataalamu kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi, Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Msalaba Mwekundu, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Hospitali ya Mifupa (Moi) na washirika kutoka nchi za Australia na Marekani. “Tulitakiwa kutoa mafunzo kwa wasaidizi 90 lakini tumetoa kwa wataalamu 104, pia tulitakiwa kutoa mafunzo kwa wataalamu wa kupokea simu 20 lakini waliopata mafunzo ni 25 na wataalamu kutoka ngazi ya jamii waliopata mafunzo ni 287 kutoka 30 pamoja na wakufunzi,” alisisitiza.Dk Sawe alisema changamoto waliyokabiliana nayo wakati wa mafunzo ni kuchelewa kwa vifaa vya kitaalamu vya kutolea mafunzo, magari ya dharura na kupendekeza wataalamu wa manunuzi kuhakikisha magari na vifaa vinatolewa ili viweze kutumika kwenye mradi. Mkuu wa Idara ya Tiba ya dharura Muhimbili, Dk Juma Mfinanga alisema huduma ya dharura ilianza rasmi nchini 2010 na wataalamu 39 wamepatikana kutoa huduma hizo na kuongeza kuwa serikali inaendelea kuhakikisha kila hospitali ya mikoa, rufaa na vituo vya afya vinakuwa na huduma hiyo.“Tafiti zinaonesha kuboreshwa kwa huduma za dharura hupunguza vifo vya majeruhi kwa asilimia 48. Tanzania imekuwa nchi ya kuigwa kwani nchi nyingi za Afrika Mashariki zimekuja kupata mafunzo ya ubingwa,” alisema Dk Mfinanga. Makamu Mkuu wa Muhas, Profesa Andrea Pembe alisema wameandaa mitaala ya aina tano ya kutoa mafunzo ya muda mfupi kuhusu huduma za dharura na wanaamini yataleta mabadiliko ya utoaji huduma za ajali na kuendelea kutoa mafunzo kutaongeza wataalamu na kuimarisha utoaji wa huduma hizo nchini.
3
WATU sita wamekufa na wengine 24 wamejeruhiwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga baada ya gari aina ya Toyota Land Cruiser kugongana uso kwa uso na gari aina ya toyota Hiace iliyokuwa imewabeba watu hao.Waliokufa ni Buruani Haule (32) na watoto wadogo watatu wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka mitatu hadi mitano ambao hawajatambulika kwa majina na wazazi wao.Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga, Richard Abwao amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo jana ambapo alisema tukio hilo limetokea majira ya saa moja na nusu katika kijiji na kata ya Nyabura barabara ya Kahama kwenda Kakola.Kamanda Abwao alisema kuwa watu sita wakufa papo hapo na 24 kujeruhiwa baada ya dereva aliyefahamika kwa jina moja la Enock (32) aliyekuwa anaendesha gari lenye namba za usajili T 710 AZZ Toyota Hiace kugongana uso kwa uso na gari lenye namba za usajiri T477 ATC Toyota Land Cruiser likiendeshwa na Thomas Evarist.Amewataja majeruhi hao kuwa ni Shabani Musa (42) ambaye amepata majeraha kichwani, Pambe Bukeleba (54) mkazi Nyakato Kahama amepata majeraha kichwani na Maria Staroni (33) mkazi wa Kahama Mjini ameumia ameneo ya kichwani.Wengine ni Mazwa Samson (41) mkazi wa Bukamba ameumia kichwani, Johari Abasi (38) mkazi wa Mwime ameumia kichwani, Thomas Katoto (32) mkazi Kahama Mjini amevunjika mkono wa kulia, Nyangige Malaki (48) ameumia kichwani, Sara Samweli (25) na Shabani Selemani 27 mkazi wa Nyahanga wameumia kichwani na mkononi.Pia wapo Anastazia James (21) mkazi wa Masumbwe aliyebainika kuvunjika mguu wa kushoto, Editha Faustine umri wa mwaka mmoja na miezi minane, pia mwanamke mmoja ambaye hakuweza kutambulika kwa jina wala makazi.
3
AGIZO la Rais John Magufuli la kutaka kila kijiji kupata umeme, limeungwa mkono na Mtanzania anayeishi nchini Poland, Julius Zellah, ambaye amejitolea kuzalisha nishati ya umeme katika eneo la Ilungu, Mbeya Vijijini.Kampuni ya Mtanzania huyo, ya Texpol Development Company (TDC) Limited, kwa kushirikiana na Light for Africa ya Poland ambayo ni taasisi ya Diaspora wa Tanzania nchini humo, zimechukua hatua ya kusaidia wananchi waishio katika vijiji vya eneo hilo kuwa na umeme, unaotokana na maporomoko ya maji kwenye mito mikubwa na milima.Akizungumza kutoka Poland, Zellah ambaye ni mlezi wa mradi huo, anasema wamepania kumsaidia Rais Magufuli na Waziri wa Nishati, Dk Merdad Kalemani. Anampongeza Rais Magufuli, kwa hatua anazochukua za kuhakikisha wananchi wanyonge na wenye kipato cha chini, wanapata umeme ili uwasaidie kurahisisha huduma za jamii, ikiwemo zahanati na shule na kwa ajili ya uzalishaji mali, kama viwanda vidogo. Zellah anamuomba Dk Kalemani kutembelea Ilungu, kukagua mradi ulipoishia na kumalizia vijiji vilivyobaki ili wananchi wapate nishati hiyo waliyoisubiri tangu uhuru. Anasema ni faraja kubwa kwa Serikali kuona wananchi hao wanatoka kwenye giza na kupata mwanga.Zellah amewajengea bure chanzo cha umeme wananchi wa vijiji 10 vya Kata ya Ilungu katika Wilaya ya Mbeya Vijijini, bila kutumia fedha za serikali. Anasema huo ni mchango wake kwa serikali ambayo imepania kujenga viwanda. Vijiji vilivyopata umeme ni Ifupa, Shango, Itiwa, Mwela, Mashese, Ngole, Nzumba, Isyonje, Nyalwela A na Nyalwela B.Katika mradi huo, ameweza kupeleka umeme na maji katika Shule ya Sekondari ya Serikali ya Ilungu, shule sita za msingi na zahanati tano. Umeme huo umepelekwa pia kwenye nyumba zote za wafanyakazi wa taasisi za serikali katika kata hiyo. Kata ya Ilungu haifikiki kwa urahisi kwa sababu iko milimani, karibu meta 2,800 kutoka usawa wa bahari.Usafiri huwa ni mgumu maradufu wakati wa kipindi cha mvua. Kata hiyo ya Ilungu iko umbali wa kilometa 52 kutoka Mbeya mjini. Ipo katika barabara inayounganisha miji ya Mbeya na Njombe na inapakana na Kata za Kitulo, Makete, Igurusi, Igoma na Irambo. Kazi ya kujenga miundombinu hiyo ya umeme,ilianza mwaka 2013 baada ya wakazi wa Kijiji cha Ifupa kumsomea risala ndefu Zellah ya kukosa umeme, ulioahidiwa na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) zaidi ya miaka 10.Mtanzania huyo aliwasihi wananchi wa kata yote ya Ilungu wasiilaumu serikali kutokana na kuwa na majuku mengi, bali wampe baraka zao aweze kuwajengea miundombinu ya kuzalisha umeme; na washirikiane naye katika kazi hiyo ngumu na yenye gharama kubwa. Hadi mwaka 2018, mradi huo ulikuwa umekamailika kwa asilimia karibu 90 na wananchi zaidi ya 16,000 wamenufaika na umeme huo.Gharama za ujenzi wa kazi hiyo hadi sasa ni takribani Sh bilioni 6.8 na utakapokamilika, itakuwa Sh bilioni 7.4. Zellah na kampuni yake ya Texpol, alikubaliana na Wakala wa Umeme Vijijini (Rea) kuwa mradi wa Ilungu utakapopatikana fedha ya serikali itaenda kuokoa maeneo mengine ya mkoani Mbeya. Baadaye ilipopatikana pesa ya serikali, Rea walitumia fursa hiyo kusambaza umeme katika Wilaya ya Chunya, kitu ambacho ni faida kubwa kwa Serikali ya Tanzania.Baada ya kumaliza usambazaji umeme, Zellah alianza jitahada za kujenga umeme wa maji kwa kutumia maporomoko ya Mto Ishinga, nje kidogo ya Kijiji cha Mwela. Ili kufanikisha kazi hiyo, kampuni hiyo ya Texpol ikishirikiana na taasisi ya Light for Africa Foundation kutoka Poland, inayounga mkono mradi huo, walianza kutafuta vyanzo vya fedha kutoka taasisi za fedha Poland.Walilenga kukamilisha umeme kwenye maeneo mengine ya vijiji vya Kata ya Ilungu na uliobaki kuunganisha kwenye mkongo wa taifa. Vijiji vilivyobaki kuunganishwa ni Nyalwela C, Nkumburu na Mabande, vyenye watu zaidi ya 6,000. Taasisi ya Light for Africa Foundation ikiongozwa na Alicja Bajowska (Mama Waka Waka) kutoka Poland, wamesaidia miradi kadhaa ya jamii katika Wilaya ya Mbeya Vijijini, ikiwemo kupeleka majiko ya kisasa, viti na meza 200.Vingine ni vitanda 123 vya chuma kwa mabweni ya wasichana wa Shule ya Sekondari ya Serikali ya Ilungu, ambako kwa muda mrefu wanafunzi walikuwa wanalala sakafuni na kusababisha waugue kila mara. Pia, taasisi hiyo imepeleka vifaa vya afya 500 (mama kit) vya kisasa vya kusaidia akina mama wakati wa kujifungua. Mwaka juzi Balozi wa Poland nchini Tanzania, Dk Ewelina Lubieniecka alimkabidhi vifaa hivyo Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Vijijini. Miundombinu ya usambazaji wa umeme ni sehemu ya kuendeleza mradi wa umeme wa maji wa karibu megawati 6.5 katika Kata ya Ilungu, uliobuniwa na kampuni ya Texpol Development Company (TDC) Limited, ikisaidiwa na Light for Africa.Lengo la kuendeleza mradi wa nguvu ya maji ni kuwezesha wananchi wa Kata Ilungu, kupata umeme wa gharama nafuu ili waanzishe viwanda vidogo kama vile useremala, kusaga nafaka, kuchomelea milango na madirisha, kutunza vyakula na kuendesha kwa ufanisi shule na vituo vya afya. Umeme wa maji utasaidia pia kurudisha gharama kubwa, zilizotumika kujenga miundomninu ya umeme kwa kata nzima.Ikumbukwe kuwa, tangu mwaka 2003, wananchi wa Kijiji cha Ifupa Kata ya Ilungu, wamekuwa wakiomba umeme kutoka Tanesco na kuahidiwa kupata nishati hiyo huku wakitakiwa kufanya kutandaza nyaya (wiring) katika nyumba zao. Baadhi walitandaza nyaya hizo, lakini hadi 2013 TDC ilipokubali mchakato wa kujenga mradi wa umeme, wakawzi walikuwa hawajapata umeme kutoka Tanesco.Wakati utafiti wa uwezekano wa mradi wa umeme wa maji unaendelea, TDC iliona kuwa ni busara kujenga miundombinu ya usambazaji karibu na eneo la mradi ili umeme huo usaidie pia wananchi. hadi makala haya yanakwenda mitamboni, Texpol bado haijamaliza mradi wake kutokana na pesa yote kutumika kwenye miundombinu ya umeme huo. Kampuni ya Texpol ilihamasishwa na wananchi wa kata nzima na ikatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya usambazaji umeme. Pesa hiyo ilitoka ndani na nje ya nchi, hasa Poland anakoishi Mtanzania huyo, Zellah, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Diaspora Tanzania nchini Poland.Ujenzi wa miundombinu hiyo ulianza kwa kilovoti 33 kutoka mkongo wa Tanesco unaotoka Mbeya kwenda Makete na kupeleka umeme huo hadi Kijiji cha Ifupa na baadaye, kata nzima ya Ilungu. Umeme huo ulijengwa chini ya usimamizi wa Tanesco. Texpol walilipa ada zote zinazohitajika kwa Tanesco kwa kusimamia kazi hiyo ngumu.Kampuni ya Texpol ilipata nyaraka zote muhimu za kisheria kwa kazi hiyo, ikiwemo leseni ya uuzaji umeme kutoka Tanesco. Vibali vingine vya kisheria ni kutoka Wizara ya Nishati, REA, MFA, NEMC, TANESCO, TIC na Mamlaka ya Bonde la Maji Rufiji.Zellah na Mama Waka Waka wanawataka Watanzania duniani kote, wasisubiri serikali ifanye kazi hiyo peke yake, bali waige mfano huu na kuisaidia kuzalisha umeme mbadala na kuusambaza kwa wananchi katika maeneo ambayo serikali bado haijafanya hivyo. Hatua hiyo itawezesha vijiji vyote vya Tanzania, kupata umeme kwa muda mfupi na kwa gharama ndogo.
3
KATI ya nyota wa kigeni waliokuwa na wakati mgumu mara baada ya kusajiliwa katika kikosi cha Yanga ni Obrey Chirwa raia wa Zambia na mchezaji ghali katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) akitokea Platinum ya Zimbabwe. Mkali huyo alisajiliwa kwa dola za Kimarekani 100,000 sawa na Sh milioni 200, mara baada ya kuridhishwa na ofa hiyo iliyokuwa imewekwa  mezani na klabu ya Yanga. Nyota huyo alikutana na presha kubwa kutoka kwa mashabiki wa Yanga, waliokuwa wakitaka kuona uwezo wake wa kufunga na kuipaisha klabu hiyo katika mashindano ya ndani na nje ya nchi. Presha hiyo ilimfanya nyota huyo ashindwe kung’aa na kuitwa garasa, huku wengine wakiilaumu klabu kwa kutumia kiasi kikubwa cha fedha kumsajili mpachika mabao huyo wa zamani wa FC Platinum ya Zimbabwe. Mabao nane katika orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu Tanzania Bara si haba, anaonyesha ni mshambuliaji wa daraja la juu, ila hakupewa muda wa kujifunza na kujipanga. Tayari mshambuliaji huyo hatari amefungua akaunti yake ya mabao katika Kombe la FA ambapo mabingwa hao watetezi wametinga hatua ya robo  fainali kwa kishindo, wanatarajia kushuka uwanjani kuwakabili maafande wa Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya. Mabingwa hao watetezi wametinga katika hatua hiyo baada ya kuibugiza mabao 6-1 Kiluvya United ya mkoani Pwani inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL). Anachokifanya Chirwa  hivi sasa ni kama kuwajibu mashabiki wa klabu ya Yanga kwa vitendo, kuonyesha uwezo wa hali ya juu na kuwa tegemeo katika safu ya ushambuliaji. Awali klabu ya Yanga ilikuwa ikimtegemea zaidi mshambuliaji raia wa Burundi, Amissi Tambwe, ambaye alikuwa akimweka benchi Mzambia huyo aliyekuwa katika kipindi kigumu. Chirwa ameanza kuandika rekodi yake ya kuwa mchezaji wa kwanza wa kigeni kufunga mabao manne katika mashindano ya Kombe la FA, ambayo yalianza kufanyika mwaka jana ambapo  Yanga walitwaa taji hilo. Uwezo wa staa huyo umekuwa juu na kuwaziba midomo mashabiki wote wenye maswali waliokuwa wakimbeza kuwa ameishiwa na hana jipya. Chirwa ni kama amezaliwa upya, amekuwa na mchango mkubwa hivi sasa na kuwa tegemeo kwa Mzambia, George Lwandamina, ambaye amekuwa akimpanga katika kikosi cha kwanza kutokana na mchango wake. Nauliza hivi kuna mtu bado ana swali juu ya uwezo wa Chirwa ambaye ametoka kuwa adui wa mashabiki hadi kuwa kipenzi cha mashabiki wa mitaa ya Twiga na Jangwani. Karibu Chirwa, karibu tena unapaswa kuwazoea mashabiki wa Tanzania ambao wapo kushangilia pekee hawajui kuwa kuna siku za kulia.
4
Mkurugenzi wa utafiti na maendeleo Kanda ya Mashariki, Tulole Bucheyeki alisema hayo hivi karibuni, mjini Morogoro katika kikao cha mpango kazi kilichowakutanisha wataalamu wa sekta ya kilimo hapa nchini. Mbegu za zao la mtama zinazofanyiwa utafiti na mradi huo ni aina ya pato, tegemeo, hakika, wahi na macia.Mratibu na mtafiti wa zao la mtama Kanda ya Mashariki, Dk Justin Ringo, alisema mradi huo umeelekeza nguvu katika mikoa na wilaya zenye ukame ambapo katika awamu ya kwanza zaidi ya wakulima 400 wanatarajiwa kufikiwa.Wataalamui hao wamesema wastani wa tani 736,000 zimekuwa zikizalishwa kwa mwaka nchini na hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi ya sita katika Afrika. Hata hivyo, wamesema juhudi zikifanyika, yapo mazingira mazuri ya kuifanya Tanzania kuzalisha zaidi ya kiwango hicho.Wataalamu hao pamoja na mambo mengine walijadili namna ya kuzalisha, kutoa na kueneza mbegu bora za zao la mtama, zao ambalo kwa sasa uzalishaji wake si mkubwa sana licha ya umuhimu wake.Bucheyeki alisema Tanzania imekuwa ikizalisha kiwango kisichoridhisha sana cha zao hilo kulinganishwa na nchi zingine za Afrika ikiwemo Nigeria ambayo ndiyo inayoongoza kwa kulima zao hilo kwa wingi.
5
NAIBU Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewaagiza watendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutoa taarifa za utekelezaji wa miradi wa usambazaji wa umeme vijijini kwa viongozi wa vijiji na wananchi wa maeneo husika ili wafahamu hatua zaidi za utekelezaji wa miradi hiyo.Mgalu alisema hayo kwa nyakati tofauti juzi wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuzindua na kuwasha umeme katika Kijiji cha Mpiji, Kata Boko katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani na kukagua maendeleo ya Mradi wa Usambazaji Umeme vijiji vya Kiluvya, Misugusugu, Mkombozi na Mtaa wa Mwambisi wilayani humo.Naibu Waziri alisema Tanesco wakiweka utaratibu wa kuzungumza na viongozi wa vijiji pamoja na wananchi mara kwa mara juu ya hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi husika, kutaondoa maswali mengi pamoja na wasiwasi walionao wananchi dhidi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo hasa usambazaji wa umeme.“Unajua Watanzania ni waelewa sana, unapompa mtu taarifa ya kile kinachofanyika katika eneo lake kwa wakati sahihi inamfanya awe na amani na waliopewa dhamana,” alisema Mgalu.Aliwaeleza Watanzania ambao hawajafikiwa na miradi ya usambazaji wa umeme kuwa na subira wakati serikali inaendelea kutekeleza kazi hiyo kwa awamu, kwa kuwa si jambo jepesi kuwafikia wananchi wote kwa siku moja.Alisema lengo la serikali ni kufikisha huduma ya umeme kwa kila Mtanzania, na kueleza kuwa serikali ilipoingia madarakani vijiji 2018 tu, ndiyo vilikuwa na umeme, sasa hivi idadi imeongezeka na kufikia zaidi ya vijiji 8,100 na tayari zaidi ya vijiji 6,000 vimeunganishwa, lengo ni kuvifikia vijiji vyote 12,319 nchi nzima ikifikapo Juni 2021.Katika mazungumzo yake na wakazi wa Kijiji cha Misugusugu, aliitaka Tanesco kuwafungia wateja, transfoma inayokidhi mahitaji ya umeme katika kijiji hicho na maeneo yanayowazunguka ili kuondoa adha ya kukatika umeme katika eneo hilo mara kwa mara ambayo inasababishwa na kulemewa kwa transfoma iliyopo.
3
KOCHA wa Yanga Charles Mkwasa amesema licha ya wao kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya JKT juzi katika mchezo wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara, kazi haikuwa nyepesi.Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Mkwasa alisema JKT sio timu ya kubeza kwa kuwa waliwapa presha baada ya kuonesha kiwango bora.Alisema anashukuru tu kuwa walipata pointi tatu na wameona baadhi ya mapungufu yao wanahitaji kuyafanyia kazi ili kuboresha na kufanya vizuri zaidi michezo inayokuja.“Pambano halikuwa jepesi, JKT sio timu ya kubeza ni timu nzuri imeimarika na ina vijana wazuri walionyesha kiwango kizuri ila tunashukuru tumepata pointi tatu na tunasonga mbele,”alisema.Mkwasa alisema kulikuwa na makosa hasa upande wa mabeki walionekana kutokuwa na mawasiliano mazuri na kipa ndio maana walitoa mwanya kwa JKT kuwafunga magoli mepesi.Alisema kwa vile bado anaendelea kuijenga timu na kuingiza falsafa yake anaamini kadiri siku zinavyokwenda mambo yatakuwa mazuri. Mchezaji huyo wa zamani wa Yanga alisema anawapa wachezaji wake siku tatu za mapumziko kisha watakutana Jumanne ili kufanya maandalizi ya muda kwa ajili ya kurekebisha mapungufu yao.
4
WATU 18 akiwemo mkuu wa shule ya Shule ya Sekondari Tumaini Lutheran Seminary iliyopo wilayani Malinyi, Mkoa wa Morogoro, baadhi ya walimu, wasimamizi wa mitihani na baadhi ya wanafunzi wamefi kishwa katika mahakama ya Wilaya ya Ulanga wakikabiliwa na makosa yanayohusu udanganyifu wa mitihani ya kidato cha nne.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Willbroad Mutafungwa alibainisha hayo jana wakati akizungumzia hatua ambazo zimechukuliwa na polisi kutokana na sakata la wizi wa mitihani ya kidato cha nne 2018.Sambamba na washitakiwa hao raia kufikishwa mahakamani, Kamanda Mutafungwa amesema pia wamemtia mbaroni askari mwenye namba G 7281 Konstebo Khamisi na kumfikisha mahakama ya kijeshi kufuatia tuhuma za kujihusisha kwake, kushiriki kwa kupanga njama na kufanya udanganyifu wa mitihani wa kidato cha nne wa shule hiyo.Alibainisha kuwa askari huyo kulingana na kanuni za jeshi atafikishwa kwanza katika mahakama ya kijeshi ili taratibu nyingine ziweze kuchukuliwa na baada ya hapo atafikishwa mahakama ya kiraia kwa mujibu wa sheria za nchi.Kwa sasa wilaya ya Malinyi bado haina mahakama ya wilaya ambapo mashauri yake yanayohusiana na ngazi ya mahakama ya wilaya yanashughulikiwa na Mahakama ya Wilaya ya Ulanga.Hivi karibuni Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), Dk Charles Msonde akizungumza Dodoma na waandishi wa habari wakati akitangaza matokeo ya kidato cha nne 2018 alisema baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali walifutiwa matokeo kutokana na kubainika kufanya udanganyifu kwa kuingia na notes ( nondo), kwenye chumba cha mtihani.Dk Msonde amesema katika hali ya kusikitisha, uongozi wa sekondari hiyo yenye namba za usajili S0983, ulionekana kupanga mbinu za ushindi kwa kuandaaa miundombinu ya kufanya udanganyifu, jambo lililolifanya Baraza la Mitihani Tanzania kufuta matokeo ya wanafunzi 57.Kwa mujibu wa Katibu Mtendaji wa Necta, walimu wote waliohusika na hujuma hiyo walikamatwa, kuhojiwa na kukiri kuhusika kwa kufanya udanganyifu katika mitihani ya masomo ya Hisabati, Jiografia, Historia na Kemia ambayo yalikuwa yameshafanyika.Dk Msonde, alizitaka Mamlaka husika ziwachukulie hatua stahiki walimu na askari polisi walioshiriki udanganyifu kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi na Sheria za nchi.Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) Januari 24, mwaka huu lilitangaza matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2018, pamoja na ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 1. 29 kutoka asilimia 77. 09 mwaka 2017 hadi asilimia 78.38 mwaka 2018.
3
Awali, Taifa Stars ilikuwa ipitie Muscat nchini Oman kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya nchi hiyo, lakini kutokana na Shirikisho la Soka la Oman kushindwa kukidhi mahitaji ya kanuni za FIFA za uandaaji wa mechi ya kimataifa za kirafiki, sasa mchezo huo hautakuwepo tena.Msemaji wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto alisema, Stars inatarajiwa kuondoka Jumapili usiku na Shirika la Ndege la Uturuki (Turkish Airlines) na kuwasili Istambul Jumatatu saa 5:00 asubuhi.Baada ya kuwasili timu hiyo itakwenda Kocael katika hoteli ya Green Park Kartepe, ambako itapiga kambi ya wiki moja kwa ajili ya kusaka makali ya kuifunga Nigeria, Super Eagles. Stars inajiandaa kufufua fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika Gabon 2017 ikiwa katika Kundi G pamoja na Nigeria, Misri na Chad.Wachezaji wa Azam FC na Yanga ambao Jumamosi wanacheza mchezo wa Ngao ya Jamii, wataungana na wenzao waliopo Stars tayari kwa safari hiyo.Aidha, taarifa hiyo ya TFF imesema kuwa mwamuzi wa kati Martin Saanya ndiye atakayechezesha mchezo wa Ngao ya Jamii kesho Jumamosi, badala ya mwamuzi Israle Nkongo aliyekuwa amepangwa awali.Nkongo anasumbuliwa na matatizo ya misuli ya paja, ambayo yatampelekea kukaa nje ya uwanja kwa siku 10, hali iliyoifanya TFF kumbadilisha mwamuzi huyo kuelekea kwenye mchezo huo wa kesho.
4
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kufungua Mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Maofisa Tawala Mikoa wapatao 52 kwa lengo la kuwapiga msasa juu ya namna ya kuongoza na kukusanya mapato.Mafunzo hayo ya uongozi ya aina yake ambayo hayajawahi kufanyika kabla, yatakuwa ya siku tano tangu leo hadi Desemba saba mwaka huu jijini hapa.Akizungumza na Habarileo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uongozi, Profesa Joseph Sembojo alisema mafunzo hayo yameandaliwa na taasisi yake kwa ushirikiano na Ofisi ya Rais-Tamisemi.Alisema ni mafunzo ya mara ya kwanza kushirikisha viongozi wa kada hiyo na hivyo yatachangia kiwango kikubwa katika kuhikisha viongozi hao wanajengewa uwezo wa kuongoza maeneo yao.Profesa Sembojo alisema mafunzo hayo yanataka kuongeza utendaji na kufanya uchaguzi na uamuzi wa mikakati, kuongoza watu na kutunza rasilimali za umma na kuwa viongozi bora katika uongozi wao.Alisema wakuu wa mikoa na maofisa tawala hao ni watu muhimu katika kuhakikisha nchini inakua kiuchumi na kimaendeleo.Alisema kutokana na programu hiyo ya nchi utawajengea uwezo wakuu hao katika kuongoza maeneo hayo lakini ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano wa Tamisemi na taasisi hiyo.Alisema mafunzo mengine kama hayo yametolewa kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi mara tano miezi ya Mei 2017 na Oktoba mwaka huu.Mafunzo hayo ya siku tano pamoja na mambo mengine masuala ya uongozi wa mtu binafsi, uhuru na mipaka ya mambo ya kisiasa, mikakati ya mawasiliano, protokali na masuala ya ulinzi na usalama, utunzaji raslimali za umma na masuala ya manunuzi na udhibiti wa dawa za kulevya katika maeneo yao.Akizungumzia mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge alisema yenye kama mwenyeji amejianda vyema kuhakikisha kwamba mkutano huo unafanikiwa.
3
Mwandishi wetu, Tanga MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema kampeni ya elimu kwa mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) itawasaidia wafanyabiashara wanaokwepa kodi kuacha vitendo hivyo vya kuikosesha Serikali mapato. Shigela ameyasema hayo ofisini kwake alipotembelewa na maafisa wa TRAwanaofanya kampeni hiyo mkoani humo ambayo imelenga kuwaelimishawafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati.  Amesema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi pengine kwa kujua au kutokua, jambo ambalo linahitaji elimu ya uelewa ili kila mwananchi afahamu wajibu wake kwenye ulipaji wa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Akiizungumzia kampeni hiyo, Shigela ameipongeza TRA kwa kuendesha zoezi hilo katika mikoa mbalimbali na kusema litaongeza ukusanyaji wa mapato baada ya wafanyabiashara kuelimishwa na kufahamu kuwa maendeleo ya nchi yanasababishwa na ulipaji wa kodi kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, barabara, umeme na maji. Shigela amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanalipa kodi kwa hiari bila kusubiri kubugudhiwa na serikali, huku akieleza kuwa serikali itaendelea kupambana na wakwepa kodi wanaoingiza bidhaa za magendo nchini kwa kupitia bandari bubu zilizopo kandokando ya Bahari ya Hindi. “Nchi yoyote haiwezi kupiga hatua ya maendeleo bila wananchi wake kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa sababu kodi ndio kila kitu huwezi kujenga barabara kama wafanyabiashara hawataki kulipa kodi, huwezi kuimarisha huduma za afya kama hakuna kodi na pia huwezi kuimarisha mifumo ya elimu bila kodi,” alisema Shigela. Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Tanga, Specioza Owure amesema kuwa, maafisa hao wa TRA wanaofanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi, watafika maeneo mbalimbali yenye wafanyabiashara katika mkoa wa Tanga na watawaelimisha kuhusu umuhimu wa kodi na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. “Maafisa hawa wanatumia jitihada zote kuwaelimisha wafanyabiashara, tunafanya hivi ili kila mmoja afahamu wajibu wake wa kulipa kodi sambamba na kusogeza huduma za TRA karibu na wateja,” alisema Owure.Kampeni ya elimu kwa mlipakodi mkoani Tanga inatarajia kumalizika Juni 30, 2020 ambapo lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara, kusikiliza maoni na changamoto zao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati.
5
NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Stella Ikupa amesema alichokipenda katika matembezi yake kwenye maonesho ya Utamaduni ya Jamafest ni kuona namna wasanii wenye ulemavu wakionesha ubunifu wao wa kutumia vifuu vya nazi kutengeneza pochi.Ikupa alitembelea maonesho hayo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana na kuwaunga mkono baadhi akisema amevutiwa na vitu vingi wanavyotengeneza akitolea mfano wa pochi hiyo sambamba na viti vilivyotengenezwa kwa kutumia vifuniko vya maji.“Nimefurahi kupata fursa ya kuja kwenye maonesho, nimeona wasanii wenye ulemavu wamefanya kazi nzuri zenye ubora natoa mwito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono kwa kuthamini vya kwetu, “alisema. Mmoja wa walemavu wa ngozi, Hadija alisema, “pamoja na ulemavu tulionao, tumekuwa tukifanya shughuli za mikono ili kujikwamua kiuchumi”. Alisema yeye licha ya kwamba ni mwanafunzi wa shahada ya pili kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii, ame- kuwa akitengeneza mapambo mbalimbali kama hereni, cheni, bangili na vitu vingine vya sanaa za mikono.Naye Boniface Kiyenze ambaye ni mlemavu wa macho alisema amekuwa akitengeneza fenicha kwa ubunifu wa kutumia vifuniko vya maji na watu wamekuwa wakivinunua na kuvifurahia.Katika hatua nyingine, Waziri huyo ameomba wadau mbalimbali kuzisaidia timu za michezo za wenye ulemavu ili ziweze kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa. Hivi karibuni Rais John Magufuli aliisaidia timu ya taifa ya soka ya watu wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’ kiasi cha Sh milioni 10 kwa ajili ya kwenda Angola kushiriki Mashindano ya Afrika.
4
WASOMI wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) wakishirikiana na Umoja wa maveterani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemuomba Rais John Magufuli kuruhusu lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia elimu ya sekondari nchini.Wasomi hao wakiongozwa na Profesa Aldin Mutembei walikutana jana Dar es Salaam na uongozi wa umoja huo uliongozwa na Mwenyekiti wake, Kapteni Mohamed Ligola. Akizungumzia jinsi walivyojipanga kufanikisha malengo hayo ya kutumia Kiswahili kufundishia nchini, Mutembei alibainisha kuwa wameanza kwa kutunga vitabu vya kufundishia kidato cha kwanza.Alivitaja vitabu hivyo kuwa ni vya siasa, fizikia, kemia, hisabati, kilimo na vingine huku akibainisha vikiruhusiwa kufundishia kidato hicho cha kwanza wawekezaji wengi watajitokeza na kuwawezesha kutunga vitabu vya kidato cha pili na kuendelea hadi vya vyuo vikuu.Alisema, tangu mwaka 2015 walishatunga vitabu hivyo na wanachosubiria kwa sasa ni ruhusa ya kuanza kutumika kwake ili ichangie kuinua kiwango cha elimu nchini. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu wa Hesabati nchini na Mhadhiri wa Hisabati UDSM, Saidi Sima aliyetunga kitabu cha hisabati kidato cha kwanza kwa Kiswahili, alisema matumizi ya lugha hiyo kufundishia itaongeza kiwango cha ufaulu nchini.Alisema, nchi itaendelea zaidi na kubainisha kuwa mwaka 1973 vitabu vya masomo mbalimbali vilivyokuwa kwa lugha ya kiingereza vilitafsiriwa kwa kiswahili na kuongeza kuwa ni muda mwafaka wa kurejesha lugha hiyo shuleni na vyuoni.Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Veterani hao wa CCM, Ligola alibainisha, mchakato wa kuwasilisha mapendekezo hayo kwa Rais Magufuli ulishaanza na kuwa wana imani atafanyia kazi hoja hiyo. Alisema, Rais Magufuli amekuwa mstari wa mbele kuendeleza lugha ya Kiswahili na hasa kutokana na tabia yake ya kukipigania kwa kukizungumza kila mahala anapokuwapo.
3
  ISLAMABAD, PAKISTAN MAHAKAMA  imemhukumu aliyekuwa waziri mkuu wa Pakistan Nawaz Sharif kifungo cha miaka 10 gerezani kwa makosa ufisadi unaohusu majengo manne ya kifahari jijini London nchini Uingereza. Nawaz Sharif,ambaye kwa sasa yuko London alihukumiwa akiwa hayuko mahakamani, na mwenyewe alisema kuwa hukumu hiyo ina mlengo wa kisiasa. Jaji Mohammad Bashir amemtaka Sharif kutumikia kifungo cha miaka 10 kwa kosa la kumiliki mali yenye gharama kubwa kuliko kipato chake na mwaka mmoja kwa kutotoa ushirikiano na mamlaka inayopambana na vitendo vya rushwa, NAB. Binti yake, Maryam Nawazi Sharif amehukumiwa kifungo cha miaka saba kwa kushirikiana na baba yake kwenye uhalifu huo na mwaka mmoja kwa kutotoa ushirikiano kwa mamlaka za kiuchunguzi huku mkwewe Nawaz akihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja kwa kutotoa ushirikiano. Sharif na Maryam wametozwa faini ya pauni milioni 8 na pauni milioni mbili. Kwa sasa wote wako jijini London ambapo mke wa Sharif, Kulsoom Nawaz anapata matibabu kutokana na maradhi ya saratani. Kashfa ya Panama Papers iliyovuja mwaka 2015 ilitoa taarifa kuwa watoto kadhaa wa Sharif walikuwa na mahusiano na makampuni yaliyo nje, ambayo yalidaiwa kupitisha fedha kwa ajili ya kununua mali nje ikiwemo majengo ya anasa jijini London. Familia yake,  inasisitiza kuwa wanamiliki mali hizo kihalali. Katika sehemu ya hukumu, Mahakama imetaka mali hizo zitaifishwe kwa serikali. Waandishi wa habari nchini Pakistani walikita kambi nje ya makazi ya Avenfield, ambako familia ilikuwa ikitazama kesi. Hukumu imetolewa wiki chache kabla ya uchaguzi mkuu wa Pakisani utakaofanyika  Julai 25  mwaka huu. Sharifu amepoteza uhalali wa kukiwakilisha chama chake cha PML-N. Kaka yake Shahbaz Sharif hivi sasa anakiongoza chama cha PML-N, na anawania katika uchaguzi huo ujao. Shahbaz amemtetea kaka yake katika mkutano na waandishi wa habari akisema kuwa hukumu hiyo ina ushawishi wa kisiasa. Mahakama ya juu ilimvua madaraka Nawaz Sharif Julai mwaka 2017 baada ya taarifa ya Panama papers. Shariff alikuwa madarakani tangu mwezi Novemba mwaka 1990 mpaka julai mwaka 1993 na kuanzia Februari mwaka 1997 mpaka alipoangushwa mwezi Oktoba mwaka 1999.  
2
SERIKALI imewataka wachezaji wa Taifa Stars kupambana kufa au kupona ili kuhakikisha wanaibuka na ushindi dhidi ya timu ya taifa ua Uganda, The Cranes, katika mchezo utakaofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.Akizungumza na wachezaji wa timu hiyo baada ya mazoezi yao jana kwenye Uwanja wa Taifa, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe aliwataka kupambana ili kuibuka na ushindi katika mchezo huo muhimu.Alisema Uganda hawana tofauti kabisa na Taifa Stars, hivyo ni matumaini yake kuwa hawatawaogopa na watacheza kufa au kupona ili kuibuka na ushindi katika mchezo huo. Alisema amefurahishwa kuona kocha wa timu hiyo Mnigeria, Emmanuel Amonike amewajengea wachezaji kujiamini na hilo linampa matumaini kuwa Uganda lazima wapokee kichapo kutoka kwa Taifa Stars.Kwa mara ya mwisho Tanzania ilifuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika miaka 39 iliyopita wakati ilipokwenda Lagos, Nigeria na tangu wakati huo imekuwa msindikizaji. Akizungumza awali na wachezaji hao, kocha Amunike amesema kutokana na aina ya wachezaji bora alionao na morali ilioneshwa nao, ana uhakika timu hiyo itaibuka na ushindi Jumapili dhidi ya Uganda.Amunike alisema kutokana na umuhimu wa mchezo huo wanatakiwa kuamini ndoto yao na kuhakikisha wanafuzu kwa fainali hizo za Mataifa ya Afrika zitakazofanyika Misri baadae mwaka huu. Alisema kuwa wachezaji wanachotakiwa ni kuweka mbele uzalendo na kuhakikisha wanapambana kufa au kupona ili kuibuka na ushindi ili kufuzu kwa fainali hizo za Afcon 2019, ambazo zitafanyika Misri. Alisema kuwa licha ya Uganda kuwa tayari imeshafuzu, lakini hilo haiufanya mchezo huo kuwa mwepesi kwani watataka kuonesha ubora wao wa kuwa kinara wa kundi hilo.“Kwa kweli Uganda ni wazuri na sisi pia ni wazuri, nimewaeleza wachezaji wangu kuwa lazima wajiamini kile wanachokifanya kwenye uwanja wa nyumbani, na lazima tuiamini ndoto yetu ya kufuzu.” Aliwahiza mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kuinga mkono timu hiyo na kwa uwezo wa Mungu watafuzu tu. “Ili kufuzu tunahitaki kuwa watulivu, kuonesha juhudi na kulenga mchezo,”alisema kocha huyo. Mwakyembe katika ziara hiyo aliongozana na viongozi mbalimbali wa michezo wakiwemo wale wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Kurugenzi ya Michezo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na wadau wengine wa soka.
4
    NA SHOMARI BINDA-SERENGETI MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan, ameuagiza uongozi wa Wilaya ya Serengeti mkoani Mara kukamilisha haraka awamu ya kwanza ya ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo ili kuondoa adha ya wananchi kusafiri kwenda mikoa mingine kupata huduma ya afya. Agizo hilo alilitoa jana mjini hapa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Mugumu wilayani Serengeti mara baada ya kutembelea ujenzi wa hospitali hiyo ya wilaya na kuweka jiwe la msingi. Alisema Wilaya ya Serengeti hupata wegeni wengi kutoka nje ya nchi, ambao wanakwenda kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, hivyo ni muhimu kwa viongozi wa wilaya na mkoa kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo kukamilisha ujenzi huo haraka ili wananchi waweze kupata huduma za afya za uhakika katika wilaya yao. “Kukamilika kwa ujenzi huo wa awamu ya kwanza kutaondoa tabu kubwa wanayopata wananchi wa Wilaya ya Serengeti katika kupata huduma ya afya karibu na maeneo yao,” alisema Samia. Katika kuunga mkono jitihada hizo za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti, Makamu wa Rais aliahidi kuchangia kiasi cha Sh milioni tano na amewaahidi wananchi wa Serengeti kuwa atahakikisha fedha kutoka serikalini ambazo zinatakiwa kupelekwa wilayani humo zinapelekwa haraka ili kukamilisha ujenzi huo.
3
Na Veronica Kazimoto, Dar es Salaam Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imewataka wamiliki wa majengo nchini kulipia kodi ya majengo ya mwaka 2017/18 hadi kufikia Juni 30, mwaka huu kwa njia ya elektroniki ambapo hakuna muda utakaoongezwa baada ya muda huo kupita. Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Charles Kichere amesema TRA haioni sababu ya kuongeza muda wa kulipa baada ya Juni 30, baada ya kuwarahisishia wamiliki kulipia kwa njia ya elektroniki badala ya kupanga foleni. “Wananchi wanaweza kupata ankara ya malipo kwa majengo yaliyosajiliwa kwenye tovuti ya TRA au simu ya mkononi na kufanya malipo katika tawi lolote la Benki ya NMB au CRDB popote nchini au kwa njia ya mitandao ya simu ya M-Pesa, Tigopesa au Halopesa. “Tunawaomba wananchi wafuatilie matangazo ya namna ya kulipa Kodi ya Majengo kwa njia ya kielektroniki katika mitandao ya kijamii na kwenye vyombo mbalimbali vya habari au wafike katika ofisi za TRA zilizo karibu na maeneo yao nchi nzima wapate utaratibu wa kulipa kodi hiyo kielektroniki,” amesema. Pamoja na mambo mengine, Kichere amesema Kodi ya Majengo inalipwa kwa mujibu wa Sheria hivyo, ni muhimu wananchi walipe mapema kodi hiyo ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza mwishoni ikiwa ni pamoja na msongamano wa watu. “Natoa wito kwa wananchi kwamba, wasisubiri mpaka mwisho ndio waanze kupanga foleni kwenye ofisi za TRA, wanatakiwa kulipa kuanzia sasa hivi katika ofisi zetu kwa kutumia njia ya kielektroniki, kinyume na hapo itatubidi tutoze faini kwa atakayechelewa kulipa,” amesema Kichere.
3
Na SOSTHENES NYONI-DAR ES SALAAM ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa  Simba, Hamis Kilomoni, amesisitiza kuwa hakubaliani na mabadiliko ya mfumo wa  uendeshaji wa klabu hiyo. Klabu ya Simba juzi ilifanya mabadiliko rasmi ya uendeshaji wake ikitoka katika mfumo wa uanachama hadi kuwa wa hisa. Mabadiliko hayo yalikuwa baada ya wanachama wa Simba  1216 kati 1217 kupiga kura ya kuunga mkono klabu hiyo kuhama kutoka mfumo wa uanachama hadi kuwa wa hisa. Mfumo huo mpya ambao umefanikisha kuundwa kwa Kampuni ya Simba Sports Club Limited, unatoa fursa kwa wawekezaji kumiliki asilimia 50 ya hisa, huku nyingine 50 zikimilikiwa na wanachama na wapenzi wa klabu hiyo. Uamuzi huo una maana ya kwamba, sasa njia ni nyeupe kwa mfanyabiashara maarufu na mwanachama wa Simba kununua asilimia 50 zenye thamani ya Sh bilioni 20. Akizungumza na MTANZANIA jana, Kilomoni alisema  aliulaumu uongozi wa Simba kwa madai kwamba umewadanganya wanachama wa klabu hiyo. “Msimamo wangu ni ule ule wa kutokubaliana na mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji ndani ya Simba, hebu fikiria wanasema watatangaza tenda wakati wanajua tayari wamempa mtu ale sasa huku si kuwadanganya wanachama wa Simba? “Kwanini suala hili wanalifanya haraka haraka kiasi hicho, kuna nini hapo, wamekutana watu elfu moja wanafanya uamuzi, Simba ina wapenzi zaidi ya milioni 20 nchi nzima, kwa jambo kama hilo walistahili kupata maoni ya watu wengi,” alisema Kilomoni. Akizungumzia kutimuliwa kwake uenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa Simba, alisema bado hajapata barua rasmi hivyo anaendelea na wadhifa wake  kama kawaida. “Sijapata barua yoyote na naendelea na majukumu yangu kama kawaida na Septemba 4 tunaenda kwenye kesi,” alisema Kilomoni. Kilomoni aliondolewa kwenye wadhifa huo na Mkutano Mkuu wa Simba uliofanyika jijini Dar es Salaam wiki moja iliyopita, huku pia akisimamishwa uanachama na kutakiwa kujieleza kabla ya kuchukuliwa hatua zaidi.
4
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi ameihakikishia jumuiya za kimataifa kuwa Tanzania itaendelea kulinda uhuru wa vyombo vya habari uliojikita katika misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, kukuza demokrasia na haki za binadamu kwa mujibu na muktadha wa nchi.Profesa Kabudi ameyasema hayo jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Balozi Malika James.Amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi chache barani Afrika na pengine duniani kuwa na vyombo vingi vya habari ambavyo vingi vinamilikiwa na watu binafsi na kwamba itaendelea kuuheshimu uhuru huo huku akivitaka vyombo vya habari navyo kuheshimu uhuru na haki za watu wengine.“Tutaendelea kuulinda uhuru wa vyombo vya habari, lakini uhuru ambao umejikita katika misingi ya Katiba yetu, pia uhuru ambao utaheshimu uhuru na haki za watu wengine,” alisema.Kuhusu suala la demokrasia nchini, Profesa Kabudi alisema Tanzania itaendelea kukuza demokrasia kwa mujibu wa muktadha na mazingira ya Tanzania ambayo huenda ikawa ni tofauti na nchi nyingine ikiwemo kutoruhusu ukabila, udini na ubaguzi wa aina yoyote, na kuwa vitu hivyo ni muhimu katika kukuza demokrasia ya nchi.“Pamoja na kwamba sisi sote ni Waafrika, ziko nchi zaidi ya 50 huku kila nchi ikifanya na kujiamulia mambo yake tofauti na nchi nyingine hivyo wasitumie vigezo na muktadha wa nchi nyingine katika kuitathmini Tanzania,” alisema.Aidha, aliongeza kuwa licha ya Tanzania kuhakikisha inaimarisha uhuru wa vyombo vya habari na kukuza demokrasia, pia inaimarisha haki za binadamu kwa kutumia taasisi zilizopo na kuruhusu uhuru wa mahakama.Katika mazungumzo hayo, wawili hao wamekubaliana kuwa mataifa hayo mawili yaendelee kujadiliana, kuzungumza, kutembeleana na kushirikiana katika nyanja mbalimbali za maendeleo kwa faida ya wananchi wa mataifa yote mawili.Profesa Kabudi alimuomba Balozi James kuhamasisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Marekani kuja kuwekeza na kufanya biashara nchini kwa kuwa mazingira ya biashara na uwekezaji yameboreshwa zaidi.Naibu Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Balozi James alieleza kuridhishwa na ufafanuzi alioupata kutoka kwa Waziri Kabudi kuhusu masuala mbalimbali hususani kukuza demokrasia, uhuru wa vyombo vya habari na kukuza haki za binadamu na kuongeza kuwa uwepo wake nchini ni katika kukuza na kuimarisha mahusiano yaliyopo baina ya Marekani na Tanzania.Aliongeza kuwa katika mazungumzo hayo, Tanzania na Marekani zimekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo katika sekta za uchumi hususani biashara, uwekezaji na usalama.Akiwa nchini, Naibu Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Balozi James amepata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki na Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
3
LEONARD MANG’OHA – DAR ES SALAAM       MWENYEKITI mpya wa Chama cha ACT Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, ameanza kazi na kutoa maazimio matano yanayohusu uendeshaji wa chama hicho na hatima ya kisiasa nchini. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Maalim Seif alisema kuwa mkutano uliofanyika mwishoni mwa wiki pamoja na mambo mengine, uliazimia kufanya maboresho ya katiba ya chama hicho ili kuongeza ufanisi na kuimarisha chama. Alisema kuwa maboresho hayo pia yanalenga kutekeleza matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya Mwaka 2019 ambayo pamoja na mambo mengine, inavitaka vyama vya siasa kurekebisha katiba zake ili kuendana na sheria hiyo. “Maboresho ya Katiba ya ACT Wazalendo, pamoja na mambo mengine yamezingatia usawa wa kijinsia na uwiano wa pande mbili za Muungano,” alisema Maalim Seif. Maalim Seif ambaye kabla ya uchaguzi huo alikuwa Mshauri Mkuu wa ACT Wazalendo, alisema kuwa mkutano huo pia ulipitia na kupitisha hesabu za chama kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita (2015-2020) na kusisitiza chama hicho kuendeleza utamaduni wake wa uwazi katika usimamizi na matumizi ya fedha za chama. “Halmashauri Kuu iliwachagua pia wajumbe wa Halmashauri Kuu, chombo cha pili kwa ukubwa baada ya Mkutano Mkuu. “Ni jambo linalotia moyo kuwa kati ya wajumbe 15 wa Halmashauri Kuu waliochaguliwa, wanane ni wanawake ambao ni sawa na asilimia 53. “Hata kwa wajumbe wa Kamati Kuu ambao jana wamechaguliwa na Halmashauri Kuu, kati ya wajumbe wanane, wajumbe wanne ni wanawake sawa na asilimia 50. “Bodi ya wadhamini ya chama chetu, ambacho ndicho chombo kikuu cha kusimamia fedha za chama, kina uwakilishi mkubwa wa wanawake kuliko wanaume. Kati ya wajumbe tisa, watano ni wanawake sawa na asilimia 55,” alisema Maalim Seif. Alisema kuwa ACT Wazalendo imethibitisha kuwa ni chama kinachojali usawa wa kijinsia kwa vitendo kwa kuwachagua na kuwateua wanawake kwenye vyombo muhimu vya kimaamuzi na nafasi mbalimbali za kimkakati. “Vijana pia wamepata nafasi ya kipekee kwenye nafasi na vyombo mbalimbali vya kimaamuzi. “ACT Wazalendo tunaamini kwamba vijana baada ya kupata malezi ya kiuongozi, wanastahili kuaminiwa kwa kupewa nafasi za kuonyesha vipaji vyao,” alisema Maalim Seif. Katika azimio la nne, alisema kuwa mkutano mkuu kwa kauli moja umeunga mkono ushirikiano wa chama hicho na vyama vingine vya siasa katika uchaguzi katika kuilinda na kuipigania demokrasia nchini. Maalim Seif alisema mkutano huo umeazimia chama hicho kishirikiane na vyama vingine makini vya siasa na makundi mbalimbali ya kijamii kutekeleza Azimio la Zanzibar la Mwaka 2018 ambalo lilisisitiza juu ya kuundwa kwa mshikamano wa makundi mbalimbali ya kijamii katika kupambana na udhalimu, dhulma na udikteta wa CCM. Kuhusu tume huru ya uchaguzi, alisema kuwa mkutano huo ulisisitiza ulazima wa chama kushirikiana na wadau wengine wa demokrasia kuipigania. “Licha ya changamoto zilizopo katika mfumo mzima wa kusimamia chaguzi zetu, mkutano mkuu uliweka bayana kuwa chama hakitasusia uchaguzi kwa sababu kwetu huu ni uchaguzi muhimu. “Kwa upande wa Zanzibar, ni dhahiri kuwa CCM imeshafahamu kuwa haiwezi kushinda uchaguzi. ACT Wazalendo tumejipanga na kujizatiti kuhakikisha kuwa tunalinda ushindi wetu kwa gharama yoyote,” alisema Maalim Seif. Kwa upande wa Tanzania Bara, alisema kuwa chama hicho kimejipanga kuhakikisha kinashinda viti vingi vya udiwani na ubunge, kuongoza halmashauri na kushirikiana na vyama vingine makini vya upinzani kuhakikisha CCM inaondoka madarakani. Katika uchaguzi huo, wajumbe wa Mkutano Mkuu waliwachagua Zitto Kabwe kuwa Kiongozi wa chama, Maalim Seif (Mwenyekiti), Dorothy Semu (Makamu Mwenyekiti Bara), Juma Duni Haji (Makamu Mwenyekiti Zanzibar) huku nafasi ya Katibu Mkuu akichaguliwa mwanasiasa kijana Ado Shaibu na manaibu wake Nassor Mazrui (Zanzibar) na Joran Bashange (Bara).
3
Na Hassan Bumbuli NAWASALIMU wapendwa wasomaji wa gazeti hili, hasa katika kipande hiki ambacho kinatupa wasaa za kuzungumzia masuala kadha wa kadha katika nyanja ya filamu hapa nchini. Nimekuwa nikiandika mambo mengi katika eneo hili na kwa hakika baadhi ya wadau wamekuwa na mrejesho mzuri kuhusu mada ninazoziandika. Yapo mengi ambayo yanaendelea kwenye filamu zetu na nimekuwa nikiyaeleza mazuri na mengine yale yenye changamoto. Leo katika makala yangu naangalia suala moja ambalo kwa sasa limekuwa kawaida kabisa kwa wasanii wetu wa kike na kiume. Hili linaweza kuwa baya na bila shaka halitawapendeza wengi, lakini ni muhimu sana tukalijadili kwa sababu lina madhara makubwa. Bila shaka katika kipindi hiki cha wiki mbili gumzo kubwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu sanaa ni ile hali ya ‘kunywa maji mengi’ iliyoibuliwa na msanii nguli wa filamu hapa nchini, Vincent Kigosi, maarufu kama Ray. Kunywa maji mengi imekuwa ni tafsiri ya kutafuta weupe, lakini kimsingi mada hiyo imekuwa gumzo kwa sababu watu wengi wamepingana na kauli ya Ray. Hakuna ubishi na inafahamika kwamba baadhi ya wasanii wetu wa filamu wamekuwa na tabia ya ‘kujikrimu’ kwa maana ya kubadilisha mwonekano wa ngozi zao ili wawe weupe. Wasanii wetu wengi hivi sasa wanajichubua kama wenyewe tulivyozoea kusema, wanataka kuwa weupe na mbaya zaidi hali hii imekuwa wa wasanii wa jinsi zote na sasa imekuwa kama ndiyo mtindo, kwani wengi sasa wanafanya shughuli hiyo. Kwani ukiwa mweusi huwezi kuigiza vizuri?  Au kuigiza kwa rangi tulizonazo ambazo tumepewa na Mwenyezi Mungu kwenye filamu tutawatisha watazamaji? Haya ni baadhi tu ya maswali ambayo nimekuwa nikijiuliza kila ninapoona filamu za baadhi ya wasanii wetu. Sasa imekuwa zaidi ya kujichubua, bali kwa vijana wa kiume ni kutafuta urembo, sizungumzii urembo wa kawaida ambao utasaidia kufanya picha zitoke nzuri, bali wasanii wetu sasa wanataka urembo wa kuonekana hata nje ya kamera, ndiyo hivyo sasa wanajichubua kabisa rangi za miili yao. Siku hizi siyo ajabu kuona filamu mbili zimeigizwa na mtu mmoja mwenye rangi mbili, kwa maana kwamba filamu ya mwezi jana alikuwa mweusi lakini ya mwezi huu, ni mweupe kushinda mzungu! Nilitegemea wasanii kuwa mstari wa mbele kukemea suala hilo, lakini utakuta msanii amechubua ngozi yake hadi mishipa ya damu inaonekana. Mbaya zaidi huo mkorogo haupitishwi pote. Unakuta mtu usoni mkorogo umekolea kwelikweli, lakini shingoni kwake ni kama amejizunguushia kaniki.     Mimi naamini kuwa msanii ni mwalimu nambari moja wa jamiii. Watu wengi wanafanya mambo kwa kuwaiga wasanii. Sasa napata shida ninapoona wasanii vijana wa kiume wanakimbilia kuweka dawa kwenye nywele, kutoga masikio na kujichumbua, maarufu kwa sasa kama kunywa maji mengi.   Ni vyema kuepukana na ulimbukeni huu, kwa wasanii ni busara wakawa walinzi wa maadili ya taifa letu kwa kuepuka kufanya mambo ambayo yanaweza kusababisha janga kubwa kwenye jamii. Tunafahamu kwamba kujichubua kunaweza kusababisha kansa ya ngozi, sasa je, wasanii wetu wanaonyesha mfano gani katika hili?   Haipendezi, tutafakari mara mbili, kwani kadri siku zinavyokwenda wale weusi watadhani kwamba kuwa mweupe ni nyongeza ya kuigiza filamu. Tujadiliane na tuelimishane kunusuru hali hii isiendelee kwa wengine na walioanza waache.
1
AJUZA Magreth Sadanda (75) analala nje baada ya kutolewa kwenye nyumba aliyojenga na mumewe kwenye kiwanja cha familia kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.Mama huyo mwenye watoto sita, anayeomba msaada kwa serikali kumsaidia kupata haki yake, aliliambia gazeti hili kuwa Desemba 19, mwaka huu, alivamiwa na watu walionunua kiwanja hicho na kumvunjia nyumba yake ya vyumba viwili na kutoa vitu nje.Akizungumzia historia yake, alibainisha kuwa alihamia Kigamboni mwaka 1977 akiwa na mumewe huyo na waliishi hapo miaka yote hadi juzi ambapo kaka wa mumewe aliposema kiwanja hicho kinatakiwa kuuzwa. Alisema kaka wa mumewe huyo aliwaahidi kuwanunulia kiwanja Mkuranga mkoani Pwani, kitu ambacho alikataa huku akisema alikuwa akitaka kupewa nauli ya Sh milioni mbili arejee kwao Mbeya.Alisema waliendelea kulumbana yeye, mumewe na shemeji yake huyo hadi wakapelekana kwenye ofisi za serikali ya Mtaa Kigamboni na uamuzi ukafikiwa kuwa apewe fedha hizi ili asafiri kwenda Mbeya. Alisema aliwapa wiki moja wamtumie fedha hizo kwenye akaunti yake ya benki ili aitumie kama nauli ya kwenda kwao, lakini wiki moja iliisha na hakukuwa fedha yoyote aliyotumiwa na matokeo yake walimvamia nyumbani hapo na kumtoa nje.Alisema, “mimi kwa kweli nimechoshwa na haya mambo nimetolewa ndani ya nyumba yangu nikiwa na watoto wangu hawa na mwisho wa siku walivunja nyumba na kutoa vyombo nje, sasa ninauliza je haki yangu ipo wapo. “Inashangaza pia hata mume wangu sijui yupo wapi kwa kuwa yeye alikuwa akikubaliana na huyo kaka yake kuwa tuhamie Mkuranga na walipokuja kuvunja na yeye aliondoka sasa sijajua ni nini kinaendelea.”Alisema inasemekana kuwa kiwanja hicho kimeuzwa kwa kitita cha Sh milioni 65 na huenda ikawa ndio sababu ya ndugu za mume wake huyo kukubali wao waondolewe kwenye kiwanja hicho. Aliwataja watoto wake hao kuwa ni Peter, Joseph, John, Pascal. Joseph aliliambia gazeti hili kuwa mbali na kuwa tukio hilo limewaletea fedheha kubwa kama familia, lakini pia limemsababisha matatizo ya kiafya mama yao.Alisema, “tunaomba Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hapa Kigamboni kutusaidia kwa kuwa kinachoonekana hapa ni kuwa haki haijatendeka kabisa na ni imani yetu kuwa serikali itasikia kilio chetu hiki.” Gazeti hili liliwasiliana na Mtendaji wa Kata ya Kigamboni, Temizigi Charles ambayo baada ya kuulizwa kuhusu sakata hilo, alienda kumtembelea Magreth na kisha kuitisha kikao cha baraza kujadili hatma yake.Alisema waliomvunjia wamekiuka taratibu zinavyotaka ya kuwa ni lazima kwanza kabla ya kuvunja nyumba au kumtoa mkazi yeyote nje ya nyumba ni lazima wahusika wawasiliane na ofisi ya kata. “Hao watu hawakufata taratibu zinavyotaka, ilikuwa ni lazima kwanza wawasiliane na ofisi ya kata ili kubainisha nini tatizo na sio kwenda kuvunja, ila ninafuatilia na nitahakikisha haki ya huyo mwanamama inapatikana,” alisema.
3
Na  PENDO FUNDISHA-MBEYA JESHI la polisi mkoani Mbeya limewafukuza kazi  polisi wawili  kwa   kukiuka maadili ya kazi baada ya kuwafanyia vitendo vibaya wanafunzi wa kike wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Isuto  iliyopo Mbeya vijijini. Askari hao ni PC Petro Mgana mwenye namba H 4925 wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Mbeya (FFU) na PC Lukas Ng’weina wa Wilaya ya Polisi Mbalizi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea November 15 usiku,   katika Shule ya Sekondari ya Isuto iliyopo Kijiji na Kata ya Isuto Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Polisi   Mbalizi. Alisema inadaiwa   askari hao kwa pamoja wakiwa kwenye ulinzi wa mitihani ya taifa ya kidato cha nne ya mwaka huu,  waliwatoa kwenye hosteli wanafunzi wa kike kwa kile walichodai kuwa walikuwa wanapiga kelele. “Baada ya kuwatoa wanafunzi hao nje, waliwapeleka eneo la foleni na kuwapa adhabu zikiwamo kupiga push up, kuruka kichura, kushika masikio na kuwachapa viboko,”alisema. Alisema  adhabu hizo ziliwasababishia maumivu makali na baadhi yao kuondoka shuleni kurudi  nyumbani kwao. “Baada ya vitendo hivyo, jeshi la polisi limewachukulia hatua za  nidhamu askari hao kwa kuwafukuza kazi kuanzia tarehe 08.11.2016 na baadaye watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika,”alisema. Hata hivyo, habari zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kwamba  Magana  amelitumikia jeshi hilo kwa miezi minne tu tangu afuzu mafunzo yake katika Chuo Cha polisi Moshi (CCP) huku Lukas akiwa amekwisha kuilitumikia kwa miaka miwili.
3
Na ADAM MKWEPU-DAR ES SALAAM IDARA ya Uhamiaji Kanda ya Dar es Salaam, imezipiga marufuku klabu za Simba, Yanga na Azam FC kuwatumia makocha na wachezaji  wa kigeni katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara hadi watakapokamilisha maombi ya vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini. Klabu hizo zinadaiwa kuwatumia wachezaji na makocha hao wa kigeni bila kuwa na vibali vya kufanya kazi wala kuishi huku wakijua kuwa ni kinyume cha sheria ya nchi. Simba imetajwa kuongoza kuwa na wachezaji wengi wasiokuwa na vibali vya kuishi wala kufanya kazi akiwamo kipa, Daniel Agyei, James Kotei, Laudit Mavugo, Mussa Ndusha, Javier Bukungu na Fredrick Blagnon. Klabu hiyo pia imetajwa kuwatumia makocha wake, Joseph Omog, Jackson Mayanja na kocha wa makipa, Iddi Salim kutoka Kenya bila ya kufuata utaratibu. Yanga wamekamilisha taratibu hizo kwa asilimia 70 huku wakituhumiwa kuwatumia makocha wake, George Lwandamina, Noel Mwandila na kiungo, Justine Zulu ambao hawana vibali vya kuishi wala kufanya kazi nchini. Tuhuma hizo pia ziliwagusa Azam kwa kuwatumia wageni 13 akiwamo beki Yakubu Mohammed, washambuliaji; Yahaya Mohammed, Daniel Amouah, Samuel Afful, Enock Agyei, wote kutoka Ghana na kiungo mkabaji, Stephan Kingue Mpondo kutoka Cameroon. Mbali na wachezaji hao, pia Idara hiyo iliwataja makocha watano ambao ni Zeben Hernandez, Yeray Romero, Jose Garcia, Sergio Perez na Joseph Nzawila pamoja na wafanyakazi wawili wa kigeni ambao hawana vibali vya kuishi wala kufanya kazi. Akizungumza na MTANZANIA jana, Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, John Msumule, alisema kuwa kwa klabu itakayokiuka agizo hilo  itachukuliwa hatua kali za kisheria ili iwe  fundisho kwa klabu nyingine zenye kuvunja sheria za nchi. “Tumechukua uamuzi huu baada ya kufanya uchunguzi na kuwahoji viongozi wa klabu husika kutokana na kuvunja sheria za nchi. “Viongozi wa Azam walisema kuwa vibali wanavyo na wanavileta leo (jana), hivyo tunawasubiri hata hivyo walisema watavileta kabla si kusubiri kufuatwa,” alisema Msumule. Msumule alisema kuwa operesheni hiyo ya ukaguzi wa vibali itakuwa ni mwendelezo ili kuhakikisha klabu zote za soka nchini zinafuata sheria na taratibu za nchi.
4
KOCHA Mkuu wa timu ya Kagera Sugar, Mecky Maxime ameahidi ushindi katika mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa CCM Kirumba hapa.Akizungumza na HabariLeo, Maxime alisema timu yake imejipanga vizuri kuhakikisha inapata ushindi katika mchezo huo ili iweze kujiweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu. Akielezea zaidi maandalizi yake, mchezaji huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars alisema wachezaji wake wote wapo fiti na tayari kwaajili ya kupindua matokeo katika mchezo huo wa leo.Alisema ligi ni ngumu sana na kutokana na msimamo jinsi ulivyo hakuna timu yenye uhakika wa kushinda moja kwa moja. Kwa mujibu wa Mecky, kwa jinsi msimamo ulivyo timu yoyote ikishinda inapanda katika ya juu na ikishuka inabakia katika nafasi za chini. Katika michezo yake saba ya hivi karibuni Kagera Sugar imeweza kushinda michezo miwili tu dhidi ya Mtibwa Sugar kwa mabao 2-1 na Lipuli FC kwa 2-0 katika uwanja wake wa Kaitaba.Timu hiyo imepoteza mechi tatu dhidi Azam kwa 2-0, Singida United kwa 2-1 na Coastal Union kwa bao 1-0. Kwa upande wake Kocha Mkuu wa timu ya Yanga, Mwinyi Zahera alisema timu yake ipo kamili kwaajili ya mchezo huo wa leo. Zahera alisema bado lengo lao la kutwaa ubingwa lipo pale pale na wana imani kubwa kuwa watalitwaa taji hilo msimu huu.
4
New York, Marekani MAREKANI imesema itazipiga marufuku kampuni 28 za China kununua bidhaa nchini humo kwa madai kuwa zinakiuka haki za binadamu na kuwanyanyasa watu wa kabila la Uighur na Waislamu wa jamii nyingine za wachache Jimbo la Xinjiang. Hata hivyo, Marekani imekanusha kuwa hatua hiyo inahusiana na mazungumzo ya biashara yaliyopangwa kuanza tena wiki ijayo. Si mara ya kwanza Marekani kuchukua hatua kama hiyo dhidi ya mashirika ya China. Mei mwaka huu utawala wa Rais Donald Trump uliiweka kampuni kubwa ya teknolojia ya Huawei katika orodha hiyo kutokana na hofu ya kiusalama kuhusu bidhaa zake. Katika vikwazo vipya, Waziri wa Biashara wa Marekani, Wilbur Ross, ameitangaza hatua hiyo akisema nchi yake haiwezi kuvumilia ukandamizaji na vitendo vya kikatili dhidi ya jamii ya walio wachache nchini China. Ross alisema marufuku hiyo itazizuia kampuni hizo kununua bidhaa za Marekani hadi kupata kibali maalumu kutoka Washington. Miongoni mwa mashirika 28 yaliyoorodheshwa ni pamoja na ofisi 18 za usalama zilizoko Xinjiang, chuo kimoja cha polisi na kampuni nane za kibiashara, ikiwemo ya bidhaa za kiteknolojia ya Hikvision na kampuni zinazoshughulika na vifaa vya ujasusi na kutambua sura ya mtu za Megvii na Sense Time. Marufuku hiyo imetangazwa huku kukiwa na mvutano kati ya Marekani na China, hasa kuhusu sera ya biashara na vitendo vinavyofanywa na China katika Jimbo la Xinjiang. Nchi hizo mbili zenye uchumi mkubwa duniani, ziko katika vita ya kibiashara, huku zikiwekeana ushuru wa mabilioni ya dola katika bidhaa zao. Jana, Ikulu ya Marekani ilitangaza kuwa mazungumzo kati ya nchi hizo yamepangwa kuanza tena Alhamisi, huku mjumbe wa ngazi ya juu wa China katika masuala ya biashara, Liu He akitarajiwa kukutana na mwakilishi wa kibiashara wa Marekani, Robert Lighthizer na Waziri wa Fedha, Steven Mnuchin. Wakati huo huo, Marekani imechukua hatua zaidi dhidi ya China kutokana na sera zake kuelekea Jimbo la Xinjiang. Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema China inawashikilia karibu Waighur milioni moja na Waislamu wengine katika kambi za ndani, ambako wanafundishwa propaganda za kikomunisti na kulazimishwa kuukana utamaduni na dini yao, kitendo ambacho Marekani inasema ni sawa na enzi za utawala wa wanazi nchini Ujerumani. Wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja mwezi uliopita, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani iliandaa mkutano kuelezea madhila wanayopitia Waighur, huku Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Sullivan akilaani kampeni ya ukandamizaji ya China ambayo ni ya kutisha. Sullivan alisema Serikali ya China inawazuia Waislamu kusali na kusoma Quran na imeivunja au kuiharibu misikiti kadhaa. Alisema huo ni mfumo unaotumiwa na chama cha kikomunisti cha China kuwazuia raia wake kutekeleza haki yao ya uhuru wa kidini. Hata hivyo, hadi hivi karibuni China imeyakanusha madai ya kuwepo kwa kambi hizo, lakini sasa imesema kuna shule za mafunzo ya ufundi, ambazo ni muhimu katika kudhibiti ugaidi, huku ikilalamikia kitendo cha kuingiliwa kwa masuala yake ya ndani. Uighurs ni kina nani? Watu wa kabila la Uighurs ni Waislamu Waturuki. Ni asilimia 45 ya watu wanaoishi Xinjiang, asilimia 40 ni watu wa kabila la Han Chinese. China ilichukua udhibiti wa eneo hilo mwaka 1949 baada ya kuliangamiza jimbo la mashariki mwa Turkestan. Tangu wakati huo, kumekuwa na uhamiaji mkubwa wa watu wa kabila la Han Chinese na Uighurs wanahofia mmomonyoko wa utamaduni wao. Xinjiang ni jimbo huru ndani ya China, kama Tibet lililopo kusini mwake.
2
KAMPENI inayohimiza watafi ti kuandika upya historia ya ukombozi wa nchi na Afrika kwa ujumla imeanza, lengo likiwa ni kuwezesha wanafunzi kusoma historia ambayo haijapotoshwa kwa makusudi.Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2019/20 bungeni jana, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (pichani) alisema mbali na wizara yake kusimamia hilo, pia itafufua kampeni ya kurejesha fuvu la shujaa Leti Hema wa Wanyaturu na mashujaa wengine lililochukuliwa na Wajerumani wakati wa ukoloni.“Wizara itahimiza kampeni... kuwezesha wanafunzi na vijana wetu kusoma historia yetu ambayo haijapotoshwa kwa makusudi na hivyo kuwajengea moyo wa uzalendo, utaifa, mshikamano, umoja na upendo,” alisema Dk Mwakyembe.Akizungumzia sekta ya maendeleo ya utamaduni, Waziri alisema baada ya kujitawala, nchi za Afrika ziliendelea kutumia vitabu vya historia, vilivyoandikwa na waliozitawala, hali iliyosababisha michango ya baadhi ya mashujaa wa harakati za ukombozi, kwa makusudi kutoakisiwa na kutothaminiwa ipasavyo.Alitoa mfano wa shujaa wa Wanyaturu, Leti aliyesimama kidete kuzuia utawala wa Kijerumani kwa zaidi ya miaka mitatu kwa kutumia makundi ya nyuki, yaliyouma wazungu pekee na kuzuia Wajerumani kukaribia kilima cha Ng’ongo Ipembe (sasa Singida Mjini) na maeneo yaliyokizunguka.“Hata alipouawa na Wajerumani baada ya kusalitiwa, wakoloni hao hawakuridhika, waliamua kukata kichwa chake na kukipeleka Ujerumani kwa uchunguzi wa kina ili kubaini kama alikuwa na uwezo maalumu wa kibaolojia wa kufundisha wadudu wenye ubongo mdogo sana kama nyuki kushambulia wazungu tu,” alisema. Kwa mujibu wa Waziri, walikwenda pia kuchunguza kuhusu muujiza aliowaonesha wa kukaa juu ya ncha kali ya mkuki badala ya kigoda cha kawaida, ali-pokutana nao kwa mazungumzo ambayo yalivunjika.Alisema shujaa huyo pamoja na wengine akiwamo Mtemi Isike wa Tabora aliyepigana na Wajerumani kwa zaidi ya miaka minne na hatimaye kuzidiwa nguvu na kujinyonga, hawajaandikwa wala mchango wao kuthaminiwa katika historia ya nchi, iliyoandikwa na wazungu. Waziri Mwakyembe alipongeza wadau wa programu hiyo, wakiwamo wabunge wanaounga mkono juhudi za kuhifadhi historia ya ukombozi wa Afrika kwa kubuni miradi mbalimbali, ikiwamo ujenzi wa makumbusho katika maeneo yaliyotumiwa na wapigania uhuru kutoka nchi za kusini mwa Afrika.
3
Tunu Nassor, Dar es Salaam Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasa), Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange, ameuagiza uongozi wa mamlaka hiyo kuongeza juhudi katika kujenga vituo vya uchakataji wa maji taka kwa maeneo ya pembezoni ili kutatua changamoto iliyopo. Akizungumza katika ziara ya Bodi ya Wakurugenzi jana, Jenerali Mwamunyange amesema mamlaka hiyo inafanikiwa kiasi kikubwa katika kupeleka maji kwa wananchi hivyo kinachotakiwa ni kuongeza vituo vya kuchakata majitaka. Amesema kuzalisha maji mengi kunahitaji pia kuweka miundombinu ya uondoshaji na uchakataji wa maji yanayotumika. “Moja ya ufumbuzi wa kupunguza tatizo la majitaka ni kujenga vituo vingi vya uchakataji kwa maeneo ya pembezoni ambalo ni jukumu la Dawasa ni kuondoa maji taka baada ya kutumika. “Hata hivyo, mamlaka ina mipango ya kujenga vituo vingi vya kuchakata majitaka karibu na wananchi jukumu ambalo limekabidhiwa watendaji wa Dawasa,” amesema.  Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Mhandisi Cyprian Luhemeja, amesema wataanza ujenzi wa vituo vya kuchakata majitaka katika maeneo ya Mashine ya Maji, Kata ya Mtoni na Mikocheni na maeneo mengine.
0
CHRISTINA GAULUHANGA Na AVELLINE KITOMARY-DAR ES SALAAM SERIKALI imesema wagonjwa wa homa ya dengue wanazidi kuongezeka na hadi sasa wamefikia 1,901 huku Kata ya Ilala, Dar es Salaam ikiongoza kwakuwa na wagonjwa 235. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi, alisema tangu watoe taarifa katika kipindi cha siku tisa, wamepata wagonjwa wapya 674. Profesa Kambi alisema ni vyema wananchi wakachukua tahadhari kwa sababu hawana uhakika kama mafuta ya nazi na majani ya mpapai yanatibu ugonjwa huo kama ambavyo wengi wanaaminishana kwa sasa. Alisema wamekuwa na wastani wa wagonjwa 75 kwa kila siku ikiwa ni tofauti na Aprili ambapo kuliwa na wastani wa wagonjwa 32. “Ongezeko hili linasababishwa na uelewa kuhusu ugonjwa huu kwa wananchi, sasa hivi wengi wenye dalili wanajitokeza kupima katika vituo vya afya na tunaendelea kufanya tathimini kama kweli mafuta ya nazi na majani ya mpapai yanatibu,” alisema Profesa Kambi. Alisema tangu kuanza kwa ugonjwa huo Januari, jumla ya watu 1,901 wamethibitishwa kuwa na virusi vya ugonjwa huo ama kati yao 1,809 wanatoka Dar es Salaam. Profesa Kambi alisema 89 walitoka Tanga huku Singida,  Kilimanjaro na Pwani walitoka mmoja mmoja. “Hakuna vifo vilivyotokea hadi sasa tangu tamko lilipotolewa Mei 10 mjini Dodoma,” alisema. DALILI ZA UGONJWA Profesa Kambi alizitaja dalili za dengue kuwa ni kupata vipele vidogovidogo, kuvilia damu kwenye ngozi na kutoka damu sehemu za fizi, ndomoni, puani, macho na kwenye njia ya haja kubwa. Alisema hadi sasa Serikali inapima ugonjwa huo bure katika vituo mbalimbali vya afya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Amana, Temeke, Mwananyamala, Sinza, Vijibweni, Mnazi Mmoja, Lugalo, Mbagala, FFU Ukonga  na vituo vya Bombo na Horohoro mkoani Tanga. “Serikali imeagiza vipimo vingine vya kupima wagonjwa 30,000  ambavyo vitasambazwa Dar es Salaam na maeneo mengine,” alisema Profesa Kambi. Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Dk. Yudas Ndungile, alisema hadi sasa vituo vya kupima ugonjwa huo kwa Dar es Salaam na Tanga vimeongezeka kutoka saba vya awali hadi kufikia 19. Alisema alili za dengue huanza kujitokeza kati ya siku tatu hadi 14 tangu mtu alipoambukizwa virusi vya ugonjwa huo. Dk. Ndungile alisema hadi sasa kuna kata 20 katika Mkoa wa Dar es Salaam ambazo zimeripotiwa kuwa na wagonjwa zaidi ya 25. Alisema kata hizo zinaongozwa na Ilala ambayo ina wagonjwa 235,  Upanga 87, Kisutu 86, Mbezi 78, Tegeta 27 na nyinginezo. Aliwataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na kuua mazalia ya mbu.
3
KATIKA kuboresha na kuinua kiwango cha ufaulu, Shule ya Msingi ya Kiislamu ya Zamzam jijini Dodoma ina mpango wa kujenga madarasa manne, yatakayowezesha watoto wa mazingira magumu kutoka mikoa mbalimbali nchini, kupata fursa ya kusoma.Akizungumza wakati wa mahojiano, Mkurugenzi wa Dalai Islamic Centre, Rashidi Bura alisema miongoni mwa mikakati waliyoiweka ni kujenga mabweni manne ili kuweza kupokea watoto kutoka mikoa mbalimbali kuanzia darasa la kwanza hadi la saba. Alisema fedha za ujenzi wanategemea kuzipata kupitia michango mbalimbali na wahisani.“Mkakati wetu ni kuhakikisha tunalea watoto katika maadili ya hali ya juu ambayo yatawasaidia kwa siku za usoni kuwa rai wema watakaolitumikia taifa kwa moyo,”alisema.Pia, alisema sasa wanajenga madarasa manne, ofisi mbili za walimu na matundu 20 ya vyoo, ikiwemo vyoo viwili kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu. Alisema kwa sasa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 350 kuanzia darasa la kwanza hadi la saba. Kati yao kuna watoto 90 ambao ni yatima na wale wanaotoka katika mazingira magumu, wanaosoma bila kulipia gharama zozote.Alisema wanafunzi wa shule hiyo, wamekuwa wakilipa ada Sh 400,000 kwa mwaka na chakula kimekuwa kikitolewa bure kwa watoto wote. Alisema shule hiyo ina uwezo wa kuchukua watoto 600 na sasa wanapokea maombi mapya na watachagua wanafunzi kulingana na idadi ya madarasa yaliyopo.Bura alitaja matatizo yao ni upungufu wa madarasa, mabweni sehemu ya kuabudia na uzio. Alisema malengo ya baadae ni kuanzisha shule ya sekondari ili wanafunzi wanapomaliza darasa la saba,waendelee na sekondari hapo.
3
Meneja Uhusiano wa Mikopo wa Kanda ya Kaskazini na Kati wa benki hiyo, Raymond Tonny alisema hayo jana alipotoa mada katika semina iliyowajumuisha wateja zaidi ya 250 kutoka Wilaya ya Babati waliounganishwa katika klabu ya biashara ya benki hiyo yenye lengo la kutoa elimu kuhusu huduma za kibenki, maboresho na kutoa mrejesho wa huduma hizo za kibenki.Tonny alisema mfanyabiashara yeyote asipotunza kumbukumbu sahihi za hesabu za biashara yake kwa huduma alizofanya za manunuzi, uuzaji na utunzaji wa mali iliyoko stoo, atajikuta makadirio yake ya kodi yatakuwa hayalingani na gharama za uendeshaji wa biashara hiyo.Alisema NMB wamekuwa wakipata changamoto hiyo kwa wateja ambao wamekuwa wana mikopo ya benki na kuhitajika kurejesha kwa wakati, ikiwa ni pamoja na riba, na baadhi yao kushindwa kulipa mikopo hiyo kwa kuwa wamelazimika kulipa tozo mbalimbali za kodi za mapato ambapo kodi hizo zipo kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi ambazo ni muhimu zikalipwa kwa maendeleo ya taifa.Tonny alitaja changamoto nyingine inayowakabili wafanyabiashara hao kuwa ni kuandaa mrithi wa biashara hizo pindi wanapougua, wanaposafiri ama kufariki hukosa mtu mwingine anayejua taarifa sahihi za biashara zao na kwamba wanapotakiwa kurejesha mikopo iliyokopwa benki wanakuwa na visingizio vingi.Kwa upande wake, Meneja wa NMB tawi la Babati, Hosea Lyatuu alifafanua kuwa benki hiyo imeboresha huduma zake, ikiwamo kufungua akaunti na huduma mbalimbali kwa lengo la kupunguza matumizi makubwa ya fedha taslimu za kubeba mkononi na badala yake kutumia huduma za kibenki katika kulipa mishahara, kuagiza bidhaa mbalimbali ukiwa unaendelea na kazi za ofisini pasipo kwenda benki.
5
CHUO Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, kimeanza ujenzi wa kiwanda cha kuchakata ngozi na kuzalisha bidhaa za ngozi katika kata ya Idifu, wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma kitakacho gharimu zaidi ya Sh milioni 500.Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Hozen Mayaya wakati wa sherehe za mahafali ya 32 ya chuo hicho Kampasi ya Dodoma, ambapo wahitimu 2,596 wametunukiwa vyeti na shahada mbalimbali."Kupitia mradi wa Eco Act, unaofadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya, Chuo kimetekeleza falsafa ya Rais Dk. John Magufuli, ya Ujenzi wa uchumi wa viwanda, chuo hiki kikikamilika kitakuwa na jumla ya wafanyakazi 70, kati ya hao 50 watakuwa wa kudumu na vibarua 20," amesisitiza Profesa Mayaya.Aidha, alisema chuo hicho kinatekeleza mradi mwingine wa kuhimili mabadiliko ya tabia nchi kwa kuzijengea uwezo Halmashauri za wilaya ya Longido, Ngorongoro na Monduli mkoani Arusha."Mradi huu ni wa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Taasisi za kimataifa za mazingira na Maendeleo (IIED), Mfuko wa Umoja wa Mataifa na Maendeleo (UNCDF LoCAL), mashirika yasiyo ya kiserikali ya Haki Kazi Catalyst (HKC) na Jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF), aliongeza Dk Mayaya.Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Mugabe Mtani, amesema utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo ya wananchi umelenga kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano iliyojipambanua kuimarisha uchumi wa nchi na maendeleo ya wananchi kwa ujumla "Katika kipindi chake cha miaka mitatu RaisJohn Magufuli, amerudisha nidhamu, uadilifu, uwajibikaji ndani ya utumishi wa umma, kuimarisha sekta ya kilimo, usafirishaji, miundombinu, na nishati" alisema Bi.Mtani Alisema hatua hiyo ya uwajibikaji wa Serikali ya Awamu ya Tano ni mafanikio yaliyofufua matumaini ya wananchi wanyonge na masikini walio wengi hapa nchini ambao wameanza kunufaika na rasilimali zao.Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Khatibu Kazungu, amekipongeza chuo hicho kwa kushiriki katika ujenzi wa viwanda hatua itakayochochea na kuiwezesha nchi kutimiza azma yake ya kuwa na uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025.Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kilianzishwa miaka 39 iliyopita na kinatoa mafunzo ya ngazi ya astashahada, stashahada, shahada na shahada ya uzamili.
5
Yanga inahitaji pointi tatu katika mechi zake tatu dhidi ya Polisi Morogoro kesho Jumatatu, Azam FC Mei 6 au Ndanda FC Mei 9, mwaka huu, kutawazwa bingwa wa Bara kwa mara ya 25, lakini vita iko katika nafasi ya pili.Ikicheza kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba iliibamiza Ndanda FC ya Mtwara kwa mabao 3-0 huku mabingwa watetezi Azam FC wakiishinda Stand United ya Shinyanga kwa mabao 4-0 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.Kwa matokeo hayo, Azam FC imeendelea kubaki katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 45 baada ya mechi 23 wakati Simba imefikisha pointi 41 katika mechi zake 24, ikibakiwa na mechi mbili, hali ambayo inatoa unafuu kwa timu ya Chamazi kupata nafasi hiyo kuliko Wekundu wa Msimbazi.Azam FC imebakiza mechi tatu dhidi ya Simba, Yanga na Mgambo JKT wakati Simba imebakiza mechi dhidi ya Azam FC na JKT Ruvu. Azam ikishinda itafikisha pointi 54 wakati Simba ina uwezo wa kufikisha pointi 47.Mabao ya Simba jana yalifungwa na Jonas Mkude katika dakika ya tisa, Ramadhan Singano katika dakika ya 15 na Said Ndemla katika dakika ya 21.Kabla ya Singano kufunga bao la pili, Ibrahim Ajibu alikosa penalti baada ya Emmanuel Okwi kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari, lakini Ajibu akapiga mpira huo wa adhabu kubwa juu ya lango la Ndanda FC ambayo iko katika nafasi ya 13 ya msimamo ikiwa na pointi 25 baada ya kucheza mechi 24.Kipindi cha pili, Ndanda FC ilicheza vizuri zaidi na kufanya mashambulizi ya nguvu langoni mwa wapinzani wao na kupata bao lililofungwa na Stamili Mbonde katika dakika ya 50, lakini lilikataliwa kwa kuwa mfungaji aliotea.Kwenye Uwanja wa Azam Complex, mabao ya wenyeji yalifungwa na Gaudence Mwaikimba aliyefunga mabao mawili, Farid Malik na bao la Mganda Brian Majwega.Majwega alifunga katika dakika ya 14 akiunganisha kwa shuti kali krosi ya Salum Abubakar, kabla ya kiungo huyo kumimina krosi nyingine iliyotumiwa vyema na Mwaikimba kuandika bao dakika ya 37.Mwaikimba, mshambuliaji wa zamani wa Yanga, alifunga bao la tatu katika dakika ya 62 akimaliza mpira uliotemwa na kipa wa Stand United, John Mwenda kutokana na krosi ya Abubakar ‘Sure Boy.’Malik aliyetokea benchi katika kipindi cha pili, alifunga bao la nne katika dakika ya 88 akimalizia kazi nzuri ya Kipre Tchetche ambaye naye aliingia uwanjani kipindi hicho cha pili.Mjini Mbeya, Joachim Nyambo anaripoti kuwa Mbeya City iliifunga Kagera Sugar kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Sokoine, huku bao la kwanza likifungwa kwa penalti na Raphael Alpha baada ya Cosmas Fredy kufanyiwa madhambi na kipa wa Kagera, Agathon Anthony katika dakika ya 45.Deus Kaseke aliwainua vitini mashabiki wa Mbeya City baada ya kufunga bao la pili katika dakika ya 55 kwa kufunga bao kwa kisigino akiunganisha pasi ya Hassan Mwasapili.Kwa matokeo hayo, Mbeya City imefikisha pointi 31 na kuchupa kutoka nafasi ya saba hadi ya tano, ikiwa imecheza mechi 24 ikibakiza mechi mbili kufahamu hatima yake katika ligi hiyo. Inafungana kwa pointi na Kagera Sugar ambayo imeng’ang’ania nafasi ya nne kwa muda mrefu sasa.
4
CHAMA cha Wanafunzi wa Kiswahili wa Vyuo Vikuu vya Tanzania (CHAWAKITA) kimetoa Tuzo ya Heshima kwa Rais John Magufuli kutokana na mchango wake mkubwa wa kuthamini na kukuza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Tanzania.Tuzo hiyo kwa Rais imetolewa na chama hicho na kupokewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kwa niaba ya Rais Magufuli. Alipokea tuzo hiyo juzi mjini Morogoro wakati akifunga kongamano la 11 la kitaifa la Chawakita lililofanyika Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro.Kongamano hilo la siku nne lilibeba kaulimbiu inayosema, “Kiswahili, Hazina ya Afrika kwa Maendeleo Endelevu” na kuandaliwa kwa tuzo kwa washindi wa uandishi wa vitabu vya hadithi fupi pamoja na ya heshima ambayo aliyotunukiwa Rais Magufuli kutokana na anavyoenzi na kukitilia maanani Kiswahili.Pia tuzo nyingine ya heshima ilitolewa kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutokana na mchango mkubwa wa wizara hiyo katika kusimamia na kuendeleza lugha ya Kiswahili nchini. Naibu Waziri Shonza baada ya kupokea tuzo hizo, aliupongeza uongozi wa chama hicho kwa kutambua umuhimu wa mchango wa Rais katika kukithamini na kukuza Kiswahili ambaye kwa sasa amekuwa ni balozi namba moja wa Kiswahili Tanzania.
3
KITENDAWILI cha mrithi wa Gadiel Michael ambaye anatajwa kutua Simba akitokea Yanga kimejibiwa kwa Yanga kumsainisha beki wa kushoto wa Malindi ya Zanzibar, Muharami Salum ‘Marcelo’.Marcelo alisaini mkataba wa miaka mitatu kuichezea Yanga juzi usiku ikiwa ni siku chache baada ya beki huyo mwenye umri wa miaka 24 kusaini mkataba wa kuichezea Singida United pia ya Ligi Kuu Tanzania Bara.“Suala la mbadala wa Gadiel limemalizika, Yanga imekubaliana na Singida United imchukue Marcelo na tayari usajili wake umeshafanyika jana (juzi) usiku. “Hakuna pengo, Marcelo ni kijana mdogo na ana uwezo mkubwa wa kufanya kazi, Yanga wajisikie wenye furaha,” alisema mtoa habari wetu.Usajili huo wa Marcelo inamaanisha Yanga sasa imeachana rasmi na Gadiel, ambaye awali ilionekana kana kwamba anaisumbua klabu hiyo katika usajili.Mwenyekiti wa Yanga, Dk. Mshindo Msolla alipoulizwa jana kuhusu usajili wa beki huyo alisema Kamati ya Usajili ndiyo yenye jukumu la kuzungumzia.Hata hivyo alikiri klabu hiyo kutafuta mbadala wa Gadiel na kwamba beki huyo ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa na nafasi kubwa ya kusajiliwa Yanga.“Ni kweli kulikuwa na mazungumzo ya kumsajili Marcelo, sijapata taarifa mpya lakini naamini wakati wowote jambo lake litamalizika au limeshamalizika,” alisema Dk. Msolla.Yanga ilishindwa kumsainisha Gadiel Michael ambaye mkataba wake wa miaka miwili ulimalizika hivi karibuni, ikidaiwa beki huyo aliyetua Yanga akitokea Azam, alikuwa hatua za mwisho za kujiunga na Simba.Wachezaji waliosajiliwa Yanga hadi sasa ni kipa wa timu ya taifa ya Kenya, Farouk Shikalo, ambapo wachezaji wengine wa kigeni ni Issa Bigirimana, Patrick Sibomana, Sadney Urikhob, Maybin Kalengo, Juma Balinya, Lamine Moro na Suleyman Mustapha.Wachezaji wazawa waliosajiliwa kabla ya Marcelo ni Ally Mtoni ‘Sonso’, Ally Ally, Mapinduzi Balama na Abdulaziz Makame.
4
Bodi ya Filamu Tanzania imemfungia muigizaji Wema Sepetu kwa muda usiojulikana.Katibu Mtendaji wa bodi hiyo, Joyce Fisoo ametangaza uamuzi huo leo jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa, Wema amewahi kuonywa lakini hajajirekebisha.Amesema, alichofanya Wema kimelidhalilisha Taifa, kimesababisha watazamaji waige tabia, mwenendo na desturi zisizofaa na kukiuka maadili yaliyo kwenye utamaduni wa Mtanzania.Fisoo amesema, Wema anafungiwa masuala ya filamu na uigizaji hadi bodi itakapojiridhisha kuwa amejirekebisha na itafuatilia kwa karibu mwenendo wake.Wema jana aliiomba radhi Serikali, Bodi ya Filamu, familia, mashabiki wake na Watanzania kwa ujumla kutokana na kosa la kusambaza video chafu kwenye mitandao ya kijamii.Tangu wiki iliyopita kumekuwa na video chafu za faragha zinamuonyesha Wema akiwa na mwanaume zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii katika kurasa za watu mbalimbali ikiwemo ya kwake mwenyewe Wema.Wema amewaeleza waandishi wa habari kuwa, anakiri kuwa amekosa kwa kuwadhalilisha na kuwafedhesha wengi akisema kilichotokea kimemuumiza na kumpa somo kubwa.“Sihitaji kumlaumu yeyote, kosa ni kosa haijalishi ilikuwaje, siombi radhi kwa kutafuta huruma ya mtu yeyote bali kukiri kuwa nililofanya ni baya. Huenda ni vitendo vya kawaida au vinavyofanywa na wote lakini vinapotoka nje huwa vinaleta taswira tofauti na isiyopendaza,” amesema.Amesema kitendo hicho ni zaidi ya aibu na kinapaswa kilaaniwe vikali na kukiri kuwa huenda anaweza asieleweke kutokana na historia ya maisha yake yaliyopita.Wema amesema, anashukuru yaliyotokea sasa kwani tangu ameingia kwenye dunia ya umaarufu mwaka 2006 alipotwaa taji la Miss Tanzania, amegundua kuwa amefanya utoto na ujinga mwingi ambao umekuwa ukiwavunja nguvu watu waliokuwa nyuma yake hata wale wasiomuunga mkono.“Kwa sababu labda sikuona athari ya vitu, na mimi naathirika vipi, lakini mara nyingi tunahitaji kufinywa ili uamke, nakiri nimefinywa hasa,” amesema na kuongeza kuwa tangu juzi amekuwa hayupo sawa akitafakari mwelekeo wa maisha yake akiahidi kutorudia makosa ya aina hiyo.
3
WAZIRI wa Nishati, Dk Medard Kalemani amepiga marufuku Shirika la Umeme nchini (TANESCO) na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kununua transfoma zinazotengenezwa nje badala yake, wanunue zinazotengenezwa nchini hususani kiwanda cha Tanelec Arusha.Waziri Kalemani alisema hayo juzi baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza transfoma cha Tanelec kilichopo jijini Arusha na kuona uzalishaji wake wenye ubora uliotukuka. Alisema kiwanda cha Tanelec kinasambaza transfoma karibu nchi nne Afrika na ni kiwanda cha kwanza Afrika kwa kutengeneza transfoma zenye ubora hivyo ni lazima serikali iunge mkono jitihada zake kwa kununua bidhaa hiyo.Alisema transfoma kutoka nje bei yake ni zaidi ya Sh milioni tisa lakini hazina ubora kama zinazotengenezwa nchini hasa kiwanda cha Tanelec ambapo transfoma moja ni Sh milioni sita. Alisema kuna viwanda vitatu vya transfoma nchini lakini kiwanda kikongwe ni cha Tanelec hivyo serikali itahakikisha inalinda viwanda hivyo kwa nguvu zote ili viwanda hivyo viweze kujiendesha na kutoa ajira kwa Watanzania.Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Tanelec, Zahir Saleh aliishukuru Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli kwa kupiga marufuku wakandarasi wa REA na mashirika mengine ya umeme kununua transfoma nje. Saleh alisema kwa uamuzi huo wa Rais, kiwanda cha Tanelec kimepata faida ya zaidi ya Sh bilioni 4 kutoka mwaka 2015 hadi sasa kwani transfoma nyingi zimekuwa zikinunuliwa na wao wameongeza uzalishaji maradufu.Alisema kila mwaka Tanelec inaongeza uzalishaji na faida nayo inaongezeka kwani mwaka 2016 kilipata faida ya zaidi ya Sh bilioni 1.2 na mwaka 2017 faida ya Sh bilioni 1.3 Akizungumzia changamoto, Mkurugenzi huyo wa Tanelec aliiomba serikali kupiga marufuku uingizwaji wa transfoma kutoka nje ya chi au kutoza ushuru mkubwa ili kulinda viwanda vya hapa nchini vinavyozalisha bidhaa hiyo.Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Bajeti waliotembelea kiwanda cha Tanelec, George Simbachawene mbali ya kuusifu uongozi wa Tanelec kwa kazi nzuri, alimshauri Waziri wa Nishati kukilinda kiwanda hicho kwa kununua bidhaa zake na kusema kuna siasa nyingi kutoka wafanyabiashara kutaka kununua transfoma nje. “Rais Magufuli amekuwa akisisitiza kulinda bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani hivyo tunapaswa kumuunga mkono kwa nguvu zote bila aibu lengo likiwa ni kupata ajira zaidi kwa Watanzania,” Simbachawene alisema.
3
*Baada ya Dimpoz, awavuta G Nako, Joh Makini CHRISTOPHER MSEKENA KATIKA ukanda huu wa Afrika Mashariki, kuna idadi ndogo sana ya wasanii wakike wanaofanya muziki wa Hip hop kwa ukubwa unaostahili. Bado haijajulikana kwanini lakini waliopo wamefanikiwa kupenya na kujitengeneza mashabiki lukuki. Mwaka 1995, huko pwani ya Mombasa, Kenya alizaliwa Petra Bockle, mrembo kutoka familia ya mama Mkenya na baba mwenye asili ya visiwa vya Seychelles ambaye kwenye muziki tunamtambua kama Petra Muzic, rapa aliyefanya unyama wa hatari, kwenye kolabo yake mpya na Ommy Dimpoz, One & Only. Nikurudishe nyuma mpaka mwaka 2018, ambapo rapa mahiri Khalighaph Jones, alimtupia mrembo huyo kwenye kolabo yao Rider, ngoma iliyovuma katika ukunda huu wa Afrika Mashariki na wapenzi wa Hip hop, wakaendelea kuupa vyeo uwezo binafsi wa Petra Muzic katika kurap, mitindo na uandishi wa mistari konki. Hivi karibuni, Petra Muzic ambaye ni mke na mama wa mtoto mmoja, alitembelea ofisi za gazeti hili na kupiga stori na mhariri wa Swaggaz, mazungumzo ambayo yalilenga kumpa nafsi ya kuendelea kujitambulisha kwa mashabiki zake wapya, maisha na mengineyo mengi, karibu. Swaggaz: Kwanini umeamua kufanya Hip hop na siyo muziki mwingine kama ambavyo wanafanya warembo wengine? Petra Muzic: Naweza kusema ni kipaji, mimi naweza kufanya vitu vingi kama kupiga ngoma, kuimba kidogo ila nimechagua kufanya muziki wa Hip hop. Swaggaz: Msanii gani wa Hip hop alikushawishi ufanye unachofanya na kwanini? Petra Music: Eminem, sababu ni mtu ambaye anaishi maisha yake kama mtu wa kawaida na ana kile kipaji cha asili ambacho Mungu amempa na huwa najiona niko kama yeye. Swaggaz: Ilikuwaje rapa mkubwa kama Khaligraph Jones kukupa kolabo? Petra Muzic: Mimi na Khaligraph tumejuana muda mrefu kabla hajawa staa na kwangu amekuwa King wa Hip hop siku zote toka kitambo. Tulianza muziki pamoja ila mimi nikaacha sababu tasnia ya muziki ya Kenya ni tofauti na Bongo kule wakisikia wewe ni noma wanakuzima. Kwa hiyo yeye aliendelea mimi nikachukua likizo ili niangalie mambo ya familia na mtoto. Kuna siku tulikutana kwenye kazi akaniambia kwende studio tukafanye kitu mnoma sana, ndiyo ikatokea ile ngoma Rider ambayo hata mama yangu anaipenda. Swaggaz: Mpango wako wa kusaidia elimu kwa wasichana hapa Afrika Mashariki umeishia wapi? Petra Muzic: Bado upo mimi nipo sana kwenye hizi kampeni za kusaidia watoto wakike, kuwainua wanawake na masuala ya kijinsia, kuna mradi nipo nao nikishirikiana na Brighter Communities Worldwide. Tumepanga kutambulisha ‘Application’ ya simu ambayo itakuwa inaunganisha wadhamini dunia nzima ambao watakuwa wanaweza ‘ku-adopt’ (kuasili) msichana kutoka kwenye hiyo ‘App’. Kwa hiyo mdhamini atapakua ‘App’ na atakutana na hao wanafunzi wasichana wenye changamoto kupitia shule zao, jambo ambalo litafanya msaada wa kielimu umfikie mhusika moja kwa moja. Kwasababu kuna shida kubwa sana Kenya na nchi zote za Afrika Mashariki, unakuta msichana anakosa shule kwasababu hana taulo za kike, watu wengi wanafanya ikiwamo serikali lakini kumekuwa na skendo za wizi, unakuta fedha zimeibiwa ila kwa hii ‘App’ utakuwa unaingia tu kama unavyoingia Instagram, kwahiyo kwa mdhamini itampunguzia matatizo ya kutuma hela bila kujua inakwenda wapi. Swaggaz: Turudi kwenye muziki, Watanzania wengi wamekufahamu baada ya kufanya wimbo na Ommy Dimpoz, mlikutana vipi mpaka mkafanya kazi? Petra Muzic: Nilikutana na Ommy Dimpoz naye akiwa kwenye  ziara ya kutambulisha wimbo wake Yanje kule Kenya, alikuwa bado mgonjwa, tulikutanishwa na mtangazaji maarufu wa Kenya, Shaffie Weru,  aliinita nikaenda, tukakutana na tukapanga namna ya kufanya na wimbo, tukaingia studio chini ya prodyuza wa Sauti Sol, One & Only ukatokea. Swaggaz: Baada ya Ommy Dimpoz kuna kolabo zingine umefanya na wasanii wa Bongo? Petra Muzic: Kolabo zipo, kuna G Nako lakini pia nimefanya kazi na Joh Makini, inatoka hivi karibuni ni wimbo mzuri wa kujibizana yaani ‘battle to battle’ siyo ngumu sana, kila mtu anaweza kusikiliza ni wimbo wa klabu. Swaggaz: Rapa gani wakike wa Tanzania unapenda kazi zao? Petra Muzic: Mimi huwa sichangui jinsia sababu mimi mwenyewe nikifanya ngoma huwa sijiangali kama msichana, huwa naangalia nani ni msanii mkali kwahiyo nawafuatilia wote wanaofanya vizuri. Swaggaz: Karibu tena Tanzania. Petra Muzic: Shukrani sana, nimewapenda Watanzania.
1
WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Yanga SC, leo watakuwa na kibarua kizito pale watakapokuwa uwanja wa Moi Kasarani, Nairobi Kenya, kucheza na wenyeji wao Gor Mahia.Yanga wataingia kwenye mchezo huo bila huduma ya baadhi ya wachezaji wake muhimu, akiwemo Kelvin Yondani na Hassan Kessy waliogoma kujiunga na kambi ya timu hiyo wakishinikiza kulipwa malimbikizo yao.Aidha, wawakilishi hao wa Tanzania pia watawakosa Mrisho Ngassa, Haritier Makambo na Deus Kaseke waliosajiliwa hivi karibuni ikielezwa hawakupata vibali kutoka kwa Shirikisho la Soka Afrika (Caf).Ushindi kwenye mchezo huo ni muhimu kwa Yanga walio kundi D ambao ndio wanashika mkia wakiwa na pointi moja huku USM Alger wakiongoza kundi kwa kufikisha pointi nne na Gor Mahia na Rayon Sports wote wakiwa na pointi mbili.Yanga walianza vibaya hatua hii ya makundi baada ya mchezo wao wa kwanza wakiwa ugenini mjini Algiers, wakicheza na USM Alger kushushiwa kipigo kizito cha mabao 4-0 kisha kutoka suluhu na Rayon kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Gor Mahia wanaonolewa na kocha wa zamani wa Simba, Dylan Kerr wataingia kwenye mchezo huo wakiwa na jeuri kufuatia kuwa washindi watatu wa Kombe la Kagame lililomalizika hivi karibuni, Dar es Salaam baada ya Juni kutwaa ubingwa wa SportPesa.Wapinzani wao walijitoa kushiriki michuano hiyo kwa madai hawakuwa na wachezaji kutokana na kukabiliwa na ukata. Akizungumzia mchezo huo, kocha mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera alisema kuwa kutokuwepo kwa wachezaji hao kumevuruga mipango yake lakini anaamini haitawaathiri.“Sio wageni kwangu nimekuwa nikiwaangalia Gor Mahia kwenye TV najua udhaifu na uimara wao, hivyo mchezo hautakuwa mgumu,” amesema Zahera.
4
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema serikali inathamini uwepo wa sekta binafsi nchini na inaendelea kushirikiana nayo katika kuboresha maendeleo ya Taifa.Aliyasema hayo jana wakati alipokutana na bodi mpya ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwenye makazi wa Waziri Mkuu, jijini Dar es Salaam.Majaliwa alimpongeza Mwenyekiti mpya wa taasisi hiyo, Salum Shamte na wajumbe wa bodi hiyo kwa kuchaguliwa kuingoza taasisi hiyo. Bodi hiyo mpya ilikwenda kujitambulisha.“Serikali ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na taasisi hii kwa sababu ndio muwezeshaji wa kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo 2025,” alisema Majaliwa.Mwenyekiti wa TPSF, Shamte alisema sekta binafsi inatambua juhudi za serikali katika kuboresha mazingira ya biashara nchini Tanzania.“Sisi tupo tayari kushirikiana na serikali kwa kuwabana wafanyabiashara ambao wanaenda kinyume na maadili na sheria, ila tunaomba serikali ishirikiane nasi katika utekelezaji wake,” alisema Shamte.Pia, Shamte aliiomba serikali iendelee kutoa vivutio kwa biashara zinazoanza ili kuhamasisha uwekezaji kwa kuwa baadhi yake zimeonesha gharama kubwa za uzalishaji.
5
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM UONGOZI wa klabu ya JKT Ruvu, umesema unakabiliwa na deni kubwa la kuhakikisha kikosi cha timu hiyo kinaimarishwa katika usajili wa dirisha dogo, ili kiweze kuanza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara kikiwa na mabadiliko makubwa. Ofisa Habari wa klabu hiyo, Constatine Masanja, aliliambia MTANZANIA jana kuwa, ripoti ya kocha Malale Hamsini ndiyo itakayowapa mwongozo katika kufanya marekebisho ambayo wanaamini yataisadia timu yao kwenye mzunguko wa pili. “Kocha tayari amewasilisha ripoti yake na tunatarajia kukutana leo au kesho kuijadili ili tuweze kuanza mchakato wa usajili kwa kuyafanyia kazi mapendekezo yake,” alisema. Alisema safu ya ushambuliaji itapewa kipaumbele katika maboresho yatakayofanywa kutokana na kushindwa kufanya vizuri katika duru la kwanza, huku akisisitiza usajili utafanywa kwa umakini mkubwa. Masanja alisema hawatabweteka katika mzunguko wa pili badala yake watapambana zaidi katika hatua hiyo ili kupata matokeo yanayoridhisha ambayo yatawawezesha kujiweka katika mazingira mazuri kwenye msimamo wa ligi.
4
Na ELIZABETH HOMBO -DAR ES SALAAM MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Chrisant Mzindakaya amesema tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961, Wizara ya Kilimo imekuwa ikiliangusha Taifa. Dk. Mzindakaya ambaye alipata kuwa mbunge wa muda mrefu aliyeingia bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 1965 akiwakilisha Jimbo la Kwela wakati huo, alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza katika mkutano kati ya Rais Magufuli na wafanyabiashara Ikulu jijini Dar es Salaam. Alisema kilimo ni sayansi na si hotuba na kwamba taasisi zote za kilimo katika wizara hiyo zinakufa.  “Kilimo ni sayansi sio hotuba tena kitaalamu, taasisi zote za kilimo katika wizara hii zinakufa na ushahidi ni Uyole-Mbeya ilikuwa inawika leo ni taabani sasa kilimo kitaendeleaje?. “Huyu waziri wako wa  Kilimo aamke nipo tayari kumshauri na hawa vijana wako wakubali  wazee tuwape ushauri naweza kusaidia bado, wala siombi kazi kwa mtu mimi, nitasaidia maana ninapenda unavyoendesha nchi,”alisema Dk. Mzindakaya. Kada huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alimshauri Rais Magufuli kutoa nafasi kwa kila waziri kuchagua jambo moja litakaloliletea sifa Tanzania kwa sababu hawawezi kufanya kila kitu. “Naamini kila mtu ana sehemu anayoiweza kwa asilimia 100 kuliko nyingine na akipewa ataifanya vizuri…kama tungetakiwa kuchagua mtu mmoja asiyefanya vitu nusunusu wewe Rais Magufuli ungepata kura nyingi za ujenzi na miundombinu kwa sababu ni kitu kilicho ndani ya damu yako hakuna anayebisha. “Sasa tunataka na mawaziri hawa uliowapa wizara angalau kila mmoja achague kitu kimoja kwa sababu hawezi kufanya yote saba,”alisema Dk. Mzindakaya. Dk. Mzindakaya aliyepata kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC), alisema mkoa wa Rukwa unazalisha mahindi kwa wingi lakini ununuzi wa mazao hayo umekuwa na siasa huku akiiomba Serikali kuwa mstari wa mbele kununua badala ya kuwaachia wafanyabiashara peke yao. “Serikali inapaswa kuchagua ni kazi gani inapaswa kufanywa na wageni pamoja na wenyeji kwa kuangalia ni nani mmiliki. “Mabilionea hawawezi kupatikana bila mpango wa Serikali wenyewe, rasimu bado ni tatizo na hakuna maamuzi ya wakati yanayotolewa kwa wafanyabishara wanapotuma maombi yao au wanapojaribu kuwasiliana na ofisi za Serikali.” “Wakati mwingine wamekuwa hawajibu barua wanazoandikiwa na wafanyabiashara na hata wanapopigiwa simu wanatuambia mzee leta nakala sasa ni mgeni gani kutoka nje atataka huo usumbufu,”alihoji Dk. Mzindakaya.
3
Mwandishi Wetu -Singida BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 katika wilaya kadhaa nchini. Misaada iliyotolewa na benki hiyo inayoongoza kwa kutengeneza faida kati ya benki zote zinazofanya biashara humu nchini ndani ya miezi mitano mwaka huu, inahusisha vifaa vya ujenzi, madawati na vifaa vingine vinavyowezesha ukamilishaji wa miradi ya afya,elimu na usalama wa raia. Benki  ya NMB imeshatoa  msaada wa  vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa mikoa ya Kanda ya Kati. Akifafanua kuhusu misaada hiyo wakati akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani ingida, Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi, alibainisha kuwa misaada hiyo ya zaidi ya Sh milioni 200 iliyotolewa imelenga sekta ya elimu, afya  na majanga kwa mikoa mitatu ya  Kanda ya kati. Akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, MkoaniSingida, katika shule ya Sekondari ya New Kiomboi, Mlozi alisema fedha hizo zilizotolewa na NMB zimetumika kununua madawati, viti vya shule za sekondari,vitanda na vifaa tiba kwenye sekta ya afya. Aidha, alisema lengo la misaada hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali. Pia alisema misaada hiyo imekabidhiwa kwa baadhi ya shule, zahanati, hospitali katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Pia NMB walikabidhi madawati 250 na vitanda 80 vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 29.5 kwa baadhi ya shule za Wilaya ya Iramba mkoani humo. Katika hatua nyingine, Benki hiyo imevipatia kituo cha Polisi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro pamoja na shule ya msingi Msowelo mabati 160 yenye thamani ya Sh5 milioni kwa ajili ya kuezekea maboma. NMB iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni mpango wa kuzipunguza baadhi ya changamoto kwa taasisi za serikali hapa nchini, Meneja wa NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus, alisema na kubainisha kuwa msaada huo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ili kusaidia kuinua miradi ya maendeleo. Baraka alisema kuwa kati ya mabati hayo, kituo cha polisi wilaya kimepa tamabati 80 huku shule ya msingi Msowelo nayo ikipata mabati 80.
5
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019  kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na  kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi  kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na  kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza.  “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake.
5
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamsaka Alex Makaptura kwa tuhuma za wizi wa ng’ombe, mali ya mfugaji mkazi wa Pongwe Musungura wilaya ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo, Makundi Steti (49).Mfugaji huyo ameibiwa ng’ombe 21 wenye thamani ya Sh milioni 5.2 waliokuwa malishoni.Aidha, mtuhumiwa huyo alikutwa na ng’ombe wengine 40, ambao walikutwa wakiwa na alama mbalimbali ikiwa inaashiria kuwa ni wa wizi.Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa. Kwamba mtuhumiwa huyo alitoroka baada ya kugundua anatafutwa na polisi.Nyigesa alisema tukio hilo ni la Aprili 27 na baada ya kufuatilia walikamata gari namba T576DEQ aina ya Toyota Hiace, ambapo walimkuta Emanuel Jonas (22) akiwa na nyama ya ngombe wawili waliochinjwa waliodhaniwa kuibiwa na alikiri kuuziwa na mtuhumiwa.“Tulipofika nyumbani kwa mtuhumiwa alitoroka na tuliwakuta ngombe hao majike yakiwa 18, madume mawili na ndama wa rika mbalimbali 20 na tulibaini kuwa ngombe hawa waliibiwa maeneo mbalimbali,” alisema Nyigesa.Alisema kuwa katika mahojiano, walifanikiwa kumkamata Shaban Kitanga, mkazi wa Manga wilaya ya Handeni mkoa wa Tanga kwa tuhuma ya kuhusika na tukio hilo la wizi wa ngombe hao 40.“Ngombe hao 40 ambao walikutwa na alama tofauti kuashiria kuwa si mali ya mtu mmoja na walipelekwa kwenye Ranchi ya Taifa ya Ruvu ili waweze kutambuliwa na wahusika,” alisema Nyigesa.Aliwataka watu waliowahi kuibiwa ngombe wao, kufika jeshi la polisi ili waonyeshwe ng’ombe hao na kuwatambua.Alitaka wananchi waendelee kutoa taarifa za uhalifu ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.
3
APRILI 26, 2018. Ni siku ya historia kwa wakazi wa mkoa wa Dodoma na Watanzania kwa jumla. Hii ni baada ya Rais John Magufuli kuitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji la Dodoma.“Nimejaribu kuangalia majiji yaliyopo nikaona kuna Jiji la Dar es Salaam, Jiji la Tanga, Jiji la Mbeya, Jiji la Mwanza, na kwa mamlaka niliyonayo kuanzia leo natangaza Dodoma siyo Manispaa tena, bali linakuwa jiji na kuanzia leo tarehe 26 mwezi huu na mwaka huu aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa atakuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma,” anasema Rais Magufuli.Siku hiyo hiyo, Rais Magufuli anaahidi kwenda kukutana na Rais wa Benki ya Maendeleo ili kuzungumza naye kwa ajili ya kupata fedha za kufanya miradi ya maendeleo kwa bajeti ya jiji badala ya kupata fedha za miradi yenye sura ya manispaa. Huo ni mwaka 2018 ulioipandisha hadhi Dodoma na kuifanya kuingia katika urithi wa matukio ya kihistoria Tanzania.Bunge lapitishaSpika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai anakaririwa na HabariLeo akisema: “Bunge litahakikisha linatengeneza Sheria ya Tamko la Dodoma kuwa Makao Makuu ambayo haitakuwa rahisi kukanyagwa kanyagwa na kubadili.”“Haijalishi kama sheria itakuwa na ukurasa mmoja, jambo la msingi kuwe na kipengele kinachotamka Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi kisheria. Suala hili limekuwa kwenye Ilani ya CCM (Chama Cha Mapinduzi) kwa miaka mingi sana, hivyo tunataka kutunga sheria ambayo siyo tu kwamba siyo rahisi kukanyagwa kanyagwa, bali pia ambayo ni vigumu kuibadili.”Huo ndio mwaka 2018 unaoelekea ukingoni. Itakumbukwa kuwa, serikali iliwasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018 uliolenga kulifanya Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Tanzania. Kupitia kwa muswada huo kunafanya sasa kuwepo Sheria ya Tamko la Makao Makuu ya Mwaka 2018 ambayo madhumuni yake ni kutangaza Jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya Tanzania.Sheria hiyo inatambua Tamko la Aprili 26 mwaka huu la Rais John Magufuli alipotangaza Manispaa ya Dodoma ambayo ni Mji Mkuu wa Tanzania kuwa Jiji la Dodoma. Pia inatambua uamuzi wa mwaka 1973, ambapo Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere alitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa makao makuu wa chama tawala; CCM na serikali. Kutungwa kwa sheria hiyo kunaifanya azma ya serikali kuhamia Dodoma kutimia na kuwa ndoto ya kweli.Asili ya Dodoma kuwa mji wa SerikaliKumbukumbu zinaonesha kuwa safari ya serikali kuhamia Dodoma ilianza tangu mwaka 1970. Lengo la safari hii lilikuwa kuutumia mji huu ulio katikati ya nchi kuwa kituo cha kuhudumia Watanzania wote au kutoa fursa kwa wananchi kutoka pande zote nchini kupata huduma za kiserikali bila kusafiri umbali mrefu. Mwaka 1973, Serikali inaamua kuanzisha Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) na kuundwa Programu ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma, ili kukidhi vigezo muhimu vya kuwa makao makuu ya nchi.Kimsingi, historia ya serikali kuhamia katika mji huyo ni ndefu na inaanza kuonesha matunda yake kamili mwaka 2016, ikiwa ni zaidi ya miaka 40, baada ya Rais John Magufuli kuweka bayana maamuzi na nia ya kutekeleza kwa vitendo azima ya serikali kuhamia Dodoma. Rais Magufuli baada ya kuingia madarakani katika anatangaza wazi kuwa Serikali itahamia Dodoma ifikapo 2020. Hatua hiyo inaondoa sintofahamu ya muda mrefu pamoja na kuwapo juhudi za serikali za kuwezesha uhamishaji makao makuu kupitia maamuzi mbalimbali ya chama tawala, Baraza la Mawaziri, nyaraka na miongozo ya serikali na matamko ya viongozi wakuu wa kitaifa.Hadi Desemba 8 mwaka huu, takwimu zinaonesha kuwa watumishi 6,531 kati ya watumishi takribani 7,000 wa wizara zote, walikuwa wamehamia Dodoma ikiwa ni sawa na asilimia 87.5 huku kundi la mwisho la watumishi 400 lilitarajia kuhamia kabla ya mwaka huu kuisha. Awamu ya kwanza ya watumishi 1,789 walihamia Dodoma mwaka 2016 wakiongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. Kisha, ikafuata awamu ya pili kati ya Novemba, 2017 ambapo watumishi 2,130 walihamia Dodoma wakiongoza na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na tayari awamu ya tatu kati ya Machi na Juni ni watumishi 2,612.Matarajio ni hadi mwisho wa mwaka 2018 zoezi la kuhamishia watumishi Dodoma liwe limekamilika na kuendelea na utekelezaji wa majukumu ya Serikali. Aidha, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi anabainisha kuwa hakuna mtumishi aliyehamia Dodoma ambaye anaidai serikali fedha za uhamisho.Mji wa SerikaliSerikali inajenga mji wa serikali katika eneo la Mtumba kilomita 7 nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Ujenzi wa Mji wa Serikali unatekelezwa ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa kuhakikisha watumishi wa serikali Dodoma ili wafanye kazi katika mazingira mazuri na yenye miundombinu yote itayorahisisha utendaji kazi wa kila siku. Serikali imeshatoa takribani Sh bilioni 1 za awamu wa kwanza kwa ajili ya ujenzi wa ofisi kwa ziara zote na kazi hizo kupewa vyombo vya ulinzi na usalama, jambo ambalo linao. Wizara 21 zimeanza hatua za awali za ujenzi ikiwemo kusafisha maeneo yao, kuweka mipaka, kuchimba misingi, kumwaga zegi na wengine uwekaji wa nondo na matofali ili kuanzia Januari, wizara kadhaa zianze kuhamia katika eneo hilo.Akizungumza katika ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alipotembelea na kukagua ujenzi wa majengo ya ofisi za serikali katika eneo la Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma, Katibu Mkuu Ofisi hiyo, Maimuna Tarishi anasema hatua ya serikali kuhamisha ofisi zake katika eneo hilo ina tija hasa ukizingatia kuwa tayari asilimia 87.5 ya watumishi wameshahamia Dodoma.Mpango wa utekelezaji wa ujenzi huo kwa awamu ya kwanza umefikia asilimia 82 na unatarajiwa kukamilika Januari 2019 ambapo viongozi na baadhi ya watumishi wanapaswa kuwa wamehamia katika eneo hilo mapema mwakani. Azma ya serikali ni kuhakikisha inajenga majengo bora yenye kuzingatia mahitaji yote muhimu ikiwemo miundombinu ya umeme, maji safi na taka, teknolojia ya habari na mawasiliamo (Tehama), mawasiliano na barabara katika mji wa Serikali Ihumwa.BaloziUjerumani imekuwa nchi ya kwanza kufungua ofisi ndogo mjini Dodoma itakayofanya pia shughuli za kibalozi. Pia Umoja wa Mataifa umeshafungua ofisi yake ya mawasiliano jijini hapa. Rais Magufuli alikabidhi hati miliki za viwanja kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yenye makazi yake hapa nchini kwa ajili ya kujenga ofisi na makazi jijini Dodoma. Hatimiliki zilizokabidhiwa ni 62 za balozi za nchi mbalimbali na 5 ni za mashirika ya kimataifa. Kila kiwanja kina ukubwa wa ekari 5.Hivyo Serikali kuhamia Dodoma kutoka Jiji la Dar es Salaam ni tukio la kihistoria linalopaswa kuandikwa katika vitabu na kumbukumbu za nchi yetu ikiwa ni wazo lililoanzishwa na Baba wa Taifa (Nyerere) lililoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2016 Serikali ilipohamia rasmi Dodoma na “limetiwa mhuri mzito’ Aprili 26, mwaka huu Rais Magufuli alipoipandisha hadhi Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji la Dodoma.
3
FAINALI ya Kombe la Mapinduzi inatarajiwa kuchezwa leo katika Uwanja wa Amaan Zanzibar kwa kuzikutanisha Simba na Mtibwa Sugar kuanzia saa 2:15 usiku.Simba ilifuzu fainali baada ya kuifunga Azam FC ambayo ilikuwa bingwa mtetezi kwa penalti 3-2 baada ya kumaliza dakika 90 kwa suluhu na Mtibwa Sugar ikaotoa Yanga kwa penalti 4-2 baada ya kumaliza dakika 90 kwa sare ya 1-1.Katika historia ya michuano hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 2007, Simba imetwaa ubingwa mara tatu ambapo mara ya mwisho Simba kutwaa ubingwa wa mashindano hayo ni mwaka 2015 kwa kuifunga Mtibwa Sugar Simba na Mtibwa Sugar zimewahi kukutana fainali mwaka, 2008 na 2015 na mara zote Simba ilishinda hivyo mchezo wa leo kila timu itakuwa inahitaji kuandika historia yake.Mtibwa Sugar imewahi kutwaa ubingwa wa Mapinduzi mara moja mwaka 2010 baada ya kuifunga Ocean View ya Zanzibar lakini imefika fainali mara sita huku Simba ikicheza fainali mara saba na kutwaa ubingwa mara tatu.Akizungumza kocha msaidizi wa Simba, Suleman Matola alisema anaamini mchezo huo utakuwa mgumu kwa sababu kila timu ina wachezaji wazuri na kila timu inahitaji kutwaa ubingwa ili andike historia ya mapema mwaka 2020.“Tunajua mchezo utakuwa na ushindani lakini tumejipanga kuhakikisha tunashinda ili tuwe bingwa kwani kuna raha ya kuanza kuandika historia ya kombe la kwanza mwaka 2020 mapema,”alisema Matola Naye kocha wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila alisema malengo yao ni kutwaa ubingwa hivyo wamejipanga kuhakikisha malengo yao yanatimia “Tumejiandaa vema na malengo yetu ni kutwaa ubingwa hivyo tunaomba Mungu atuamshe salama ili tukafanikishe lengo letu,” alisema Katwila Mashindano haya ya 13 yalishirikisha timu nne za Zanzibar ambapo zote zimeaga mashindano na timu nne za Tanzania Bara na yanachezwa kwa mtindo wa mtoano ambapo bingwa anatarajiwa kuondoka Sh Milioni 15 pamoja na Kombe.Timu ambazo zilishiriki mashindano kutoka Kundi A ni na tayari zimeaga mashindano ni Yanga, Mlandege na Jamhuri na Kundi B ni timu za Azam FC, Zimamoto na Chipukizi.Mashindano hayo maalum kwa ajili ya kusherehekea miaka 56 ya Mapinduzi yalianza mwaka 2007 na hufanyika kila mwaka na mwaka huu yalichezwa kwa mtindo wa mtoano.Orodha ya Mabingwa Kombe la Mapinduzi. 2007.Yanga2008. Simba2009. Miembeni2010. Mtibwa Sugar2011.Simba2012.Azam FC2013. Azam FC2014.KCCA2015. Simba2016. URA2017. Azam FC2018. Azam FC2019. Azam FC
4
Masanii Gigy Money amesema ana wivu sana kwa mpenzi wake wa sasa na akishika tu simu inakodolea macho kama fundi saa. Katika ukurasa wa Instagram Gigy ameposti picha akiwa pamoja na mpenzi wake huyo wa sasa huku akiwa anachungulia simu yake. Binadamu tumeumbwa na wivu lakini wangu umezidi kila akishika simu mimi mijicho yangu inatoka kama nimepoteza nati ya saa.. achana na swala lakuchungulia cm ata Beyoncé anafanyaga ivi 🤣 yani mapenzi ayana mazoea nikulinda mzigo wako tu ❤️ wivu kidonda 🤦🏻‍♀️ @hunchyhuncho najua ujaelewa ila jua Nakupenda sana ❤️❤️❤️🥰 A post shared by 𝐊𝐢𝐤𝐢 𝐍𝐢 𝐆𝐢𝐠𝐲 🇹🇿 (@gigy_money_og) on Jan 20, 2020 at 10:32pm PST Amesema binadamu wote wana wivu ila wa kwake umezidi na mapenzi hayana mazoea kikubwa kulinda mzigo wako, “Wivu ni kidonda”. Gigy sasa ni mtu wa kula bata nchi za nje na huyo mpenzi wake ambaye ameamua amkabe mpaka penati. Ana Tamani niwe wake ….. akiniona niko Nawe akithubutu anifate ukimuona rusha mawe Zaddy 💕💓 my life is nothing without you ❤️ A post shared by 𝐊𝐢𝐤𝐢 𝐍𝐢 𝐆𝐢𝐠𝐲 🇹🇿 (@gigy_money_og) on Jan 18, 2020 at 5:44am PST
1
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
NA ALOYCE NDELEIO, UCHAGUZI wa Marekani  lilikuwa ni tukio moja ambalo lilitawala nyanja nzima ya habari hususani baada ya matokeo yake  kutangazwa na  kuibua picha tofauti na matarajio ya walio  wengi. Aidha wale wanaoegemea kutabiri masuala ya siasa za Marekani walibakia  kuegemea  umaarufu ambao uongozi unaomaliza muda wake  umejipatia  katika Afrika, hawa waliduwazwa; wale wanaoielewa sura ya kinyonga ya Marekani  hawakushangaa kuyaona mabadiliko yaliyotokea. Kwa upande mwingine  matamanio na matarajio ya  watu na hususani miongoni mwa nchi za Afrika  walikuwa  upande wa Democrat taswira  ambayo inaweza kuelezwa kuwa ni kutokana na kudekezwa na uongozi unaomaliza muda wake na hususani kwa mtazamo wa masuala ya ‘Kwa  hisani ya watu wa Marekani.’ Wale wanaozielewa siasa  za Marekani  ni kwamba haziwezi kushabikiwa kama ligi ya soka ya Ulaya, au kule Marekani kwenyewe katika ligi ya Mpira wa Vikapu ya NBA. Kilichojitokeza na ambacho kinaweza kuelezwa kuwa  tukio la ajabu ni ile taarifa kwamba  wabunge  wanawake wa Tanzania  wamesikitishwa na kushindwa kwa mgombea  urais wa Marekani  kwa tiketi ya Democratic, Hillary Clinton. Kauli hiyo  inatosha kuwafikirisha wavuja jasho na kuipata picha halisi kwamba ni upande upi wanawake hao walikuwa wameuegemea katika mtazamo na matamanio yao katika Uchaguzi Mkuu wa Marekani. Kama  ujumbe huo wa kusikitishwa na matokeo hayo miongoni mwa wabunge wanawake wa Tanzania  ulimfikia  au la, hilo wavuja jasho hawawezi kulifahamu. Lakini kama  ujumbe huo ulimfikia wavuja jasho wanavuta  hisia tofauti. Kwa mbali hisia  za wavuja jasho zinakutana na mwangwi wa sauti ikisema, “Msinililie mimi enyi wanawake wa Bongo, jililieni wenyewe na muwalilie wenzenu ambao hamuwaungi mkono  katika chaguzi zenu.” Kwa upande mwingine inaweza kuelezwa kuwa wabunge hao hawajawaona wanawake waliogombea nfasi za uongozi nchini mwao na ambao  huenda walishindwa kutokana na kutoungwa mkono na wanawake wenzao. Kwa kuangalia uhalisia hali hiyo inaonesha unafiki  uliomo ndani ya wanasiasa wanawake kwa kuwa  katika Uchaguzi Mkuu  wa mwaka jana  wa Rais na wabunge na madiwani  walikuwapo wanawake waliogombea nafasi mbalimbali na hata nafasi ya Urais. Pamoja na hali hiyo wapo wanawake pia waliotangaza nia na kuchukua  fomu za kugombea nafasi hiyo na hata kufikia hatua za mchujo  ambapo majina yao yalikatwa. Hoja ni wanawake wangapi  miongoni mwao hadi  leo wameshaonesha kusikitishwa  kushindwa  katika uchaguzi huo kwa wanawake wenzao? Leo hii wamekuwapo wanawake  ambao  pamoja na  kushinda  uchaguzi  huo  katika ngazi ya ubunge, wapinzani wao  wamefungua  kesi mahakamani kupinga  ushindi wao. Mmojawapo ni Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya  ambaye katika kesi  zilizofunguliwa katika mahakama ngazi tofauti ameshinda kesi yake  dhidi ya mpinzani wake Mzee Steven Wassira. Hoja ni wanawake wangapi  wameweza kujitokeza hadharani kumlilia katika mapambano yake ya kesi hiyo  na walau hata kumpongeza hadharani kama ambavyo wangetarajia kumpongeza Clinton iwapo angeshinda? Inapotokea wachambuzi wa mambo wakasema kuwa  baadhi ya akili za wanasiasa  na hata baadhi ya wasomi wetu zimehamishiwa Ughaibuni nani atakataa uhalisia huo kwamba hawaoni yaliyomo ndani  mwao bali kwa wenzao? Je, wabunge hao wanawake hivi kweli walimsikitikia Anna Mghwira  aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya  ACT – Wazalendo kwa kushindwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita? Upo usemi hisani huanza nyumbani  lakini hilo  kwa wanasiasa hao halifahamiki ila lililo muhimu kwao labda ni lile ambalo linatokana na ‘Kwa hisani ya watu wa Marekani.’ Si ajabu kwamba  hivi sasa wapo katika matamanio ya kinjozi kwamba kura hizo zikirudiwa kuhesabiwa Clinton ataibuka mshindi. Haiyumkini hawa wanatakiwa kutoa boriti jichoni ndipo waone vibanzi hivyo vilivyopo Ughaibuni.
3
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
Na Christian Bwaya TUMEKUWA tukisikia matukio ya watoto kudhalilishwa na watu wao wa karibu. Hapa tunazungumzia matukio kama kuingiliwa kimwili, kushikwa isivyo stahili, kutomaswa na vitendo vingine vinavyoashiria ngono. Matukio kama haya huwaathiri mno watoto kimwili, kisaikolojia na hata kiroho. Watoto wengi wanaoingiliwa kimwili, kwamfano, hujenga hofu, hushindwa kuwaamini tena watu ambao kimsingi wangepaswa kuwaamini, hujichukia na matokeo yake mtazamo wao kuhusu wao na maisha kwa ujumla hubadilika. Tafiti zinaonesha kuwa mara nyingi matukio haya huhusisha watu wanaoishi na mtoto. Hawa ni watu ambao kwa namna moja au nyingine walitarajiwa kuwa walinzi wa mtoto ndio hao hao wanaogeuka kuwa watu hatari kwa ustawi wa mtoto. Ikiwa unataka kuwalinda watoto na vitendo hivi, unayo kila sababu ya kutambua viashiria vya hatari kwa mtoto ili uweze kuchukua hatua stahiki kabla mambo hayajawa mabaya. Makala haya yanaangazia baadhi ya viashiria vya hatari kupima kiwango cha usalama katika ngazi ya familia. Mtoto anamwamini nani? Kama nilivyotangulia kusema, mara nyingi mtu anayeaminiwa na mtoto ndio huyo huyo anayeweza kugeuka kuwa tatizo kwa siri. Ikiwa unataka kumlinda mwanao na udhalilishaji usichukulie kirahisi rahisi imani kubwa anayokuwa nayo mwanao kwa mtu anayeishi hapo nyumbani. Wabaini watu ambao mwanao hujisikia huru kuwa nao. Anaweza kuwa baba, mjomba, msaidizi wa kazi au ndugu mwingine yeyote. Mfundishe mwanao kujenga mipaka nao. Hakikisha anaelewa kuwa pamoja na kuwapenda, bado kuna vitu hapaswi kuvifanya akiwanao. Mfano, kuvua nguo mbele yao, kuwakalia, kukaa nao mahali pa faragha. Mtoto akijenga tabia hii mapema itamsaidia kuelewa pale mtu huyo anapoanza kuvuka mipaka hiyo. Mtoto anaelewa kuhusu udhalilishaji? Matukio mengi ya udhalilishaji huanza hatua kwa hatua. Wakati mwingine mdhalilishaji humwaminisha mtoto kuwa yuko salama lakini kumbe safari ya udhalilishaji ndio kwanza inakuwa imeanza. Kukabiliana na tatizo ni muhimu kutathmini uelewa wa mtoto kuhusu udhalilishaji. Watoto wengi wanaodhalilishwa, wakati mwingine, huwa hawana uelewa wa kutosha unaosaidia kutambua hali isiyo ya kawaida. Elimisha wanao wafahamu, kwa mfano, kuwa kushikwa shikwa na mtu mwingine ni udhalilishaji. Mtu mwingine yeyote hata awe rafiki wa baba na mama hawezi kumshika kwenye maeneo Fulani ya mwili. Kuna maneno ambayo hakuna mtu anaweza kumwambia bila kujali hadhi yake na nafasi yake kwenye jamii. Mtoto anayeelewa hivyo anaweza kuwa mwepesi kutoa taarifa pale hali hiyo inapojitokeza. Mtoto huenda wapi asipokuwa nyumbani? Wakati mwingine mtoto hupata matatizo kwa sababu ameenda mahali hatarishi na mtu anayemwamini. Usipojua ameenda wapi hiyo inaweza kuwa sehemu ya tatizo. Jiulize, mtoto asipokuwa nyumbani anakuwa wapi? Je, anacheza wapi na nani? Marafiki zake wanapendelea nini? Je, anapotoka nyumbani, huambatana na mtu mzima yupi? Haya ni mambo ya msingi kuyafahamu ikiwa unalenga kumlinda mwanao na hatari ya udhalilishaji. Mtoto hulala na nani? Wakati mwingine mazingira anamolala mtoto yanaweza kuwa kichocheo cha udhalilishaji. Jiulize, nani analala na mwanao? Je, umeruhusu watoto wa kike na wa kiume kulala pamoja? Je, msaidizi wa nyumbani anayelala na mtoto ni mtu salama? Je, unaruhusu baba kulala na mwanao wa kike? Christian Bwaya ni mnasihi na mhadhiri wa Saikolojia Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge, Moshi. Wasiliana naye kwa 0754870815
0
NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM VYAMA nane vimefungua kesi katika Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ), kupinga Sheria ya Vyama vya Siasa iliyoanza kutumika rasmi mwaka huu. Vyama hivyo ni Chadema, NCCR – Mageuzi, NLD, UPDP, CCK, ACT – Wazalendo, Chaumma na DP. Akizungumza kwa niaba ya vyama hivyo, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, alisema kesi hiyo namba 3 ya mwaka 2019 imefunguliwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na tayari maombi yao yamepokelewa katika mahakama hiyo. “Tumelazimika kutafuta haki katika Mahakama ya Afrika Mashariki kwa sababu sheria hii inafanya shughuli za kisiasa nchini kuwa jinai kutokana na kila kifungu cha sheria kuweka adhabu ya faini, kifungo au vyote kwa pamoja. “Tunaiomba mahakama itamke kwamba vifungu tunavyovilalamikia havina hadhi ya kisheria,” alisema Mbowe. Alisema sheria hiyo inakiuka misingi ya uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hasa ibara ya 6, 7 na 8 ya mkataba wa uanzishwaji wa jumuiya hiyo. Mbowe alisema mbali ya kukiukwa kwa Mkataba wa EAC, vifungu vya sheria hiyo vinakiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na misingi ya utawala bora pamoja na mikataba mbalimbali ya kimataifa ambayo Tanzania imesaini. Alivitaja vifungu 11 alivyodai kuwa havina hadhi ya kisheria kuwa ni kifungu cha 3 (b), 3 (g), 5 (A) (i), 5 (B) (i), 6 B (d), 8 (C) (2), 8 D (2), 8 (E), 11 A (2), 23 (7) na 21 (E).   “Kifungu cha 3 (d) kimempa Msajili wa Vyama vya Siasa jukumu la kusimamia chaguzi za ndani ya vyama ikiwa ni pamoja na teuzi za wagombea wa nafasi mbalimbali. “Hii inampa msajili mamlaka ya kuingilia vyama na kuviamulia ni nani awe kiongozi wa chama husika au mgombea wa nafasi ya kiserikali kama mgombea urais na ubunge,” alisema Mbowe. Mbali ya kwenda Mahakama ya Afrika Mashariki vyama hivyo vilisema vinatarajia pia kufungua kesi katika Mahakama Kuu na iwapo vitashindwa vitaendelea hadi Mahakama ya Afrika. CAG na Ndugai Katika hatua nyingine, sakata la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad na Spika wa Bunge, Job Ndugai, limechukua sura mpya baada ya vyama vinane vya upinzani kumtaka spika Ndugai ajiuzulu. Juzi Spika Ndugai alisema kitendo cha Profesa Assad kuendelea kulitumia neno dhaifu ni dharau na kejeli kwa mhimili huo muhimu na kumtaka ajiuzulu kwani anampa wakati mgumu Rais John Magufuli. Akizungumza jana kwa niaba ya vyama hivyo, Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa, alisema taifa limeingizwa kwenye misukosuko bila sababu kwa utashi wa spika. “Hatua ya kumkataa CAG ni jambo ambalo utekelezaji wake una utata, Bunge linapaswa lisikilize maoni na kuzingatia hoja za wananchi. “Hatua ya Spika kutangaza kwamba CAG akamuombe radhi Rais anataka kumchanganya Rais katika mgogoro wake, atuambie anataka Rais afanye nini. Baada ya kuona ushauri wake hausikilizwi yeye angeshuka si kung’ang’ania na kugonganisha taasisi…ajiuzulu,” alisema Dovutwa. Dovutwa pia aliwataka viongozi wakubali kukosolewa na kutokuwa wakali na kusisitiza kuwa wao wanamuunga mkono CAG. “Leo amemkataa CAG, kesho anaweza kuleta hoja kumkataa Jaji Mkuu au Mkuu wa Majeshi. CAG asimamie msimamo wake, wananchi na kambi ya upinzani tuko pamoja naye,” alisema. Gazeti hili lilifanya juhudi ya kumtafuta Spika kwa njia ya simu, lakini simu yake ya kiganjani ilikuwa haipatikani. UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA Vyama hivyo vimemuomba Waziri wa Tamisemi, kuharakisha kutoa mapitio ya kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili waweze kuzipitia na kuona maeneo yanayopaswa kufanyiwa marekebisho. “Waziri afanye haraka alete mapitio ya kanuni tuyajadili na kuona ni maeneo gani yanapaswa kufanyiwa marekebisho. Tusije tukaletewa hizo kanuni zikiwa zimebaki wiki mbili au tatu,” alisema Katibu Mkuu wa Chama cha Kijamii (CCK), Renatus Muhabi.
3
MENEJA wa Maabara wa Tume ya Madini, Dornald Joseph Njonjo (30) anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa tuhuma za kuiba madini ya dhahabu kilogramu 6.244 yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 507, yaliyokuwa yamehifadhiwa kwenye Kasiki ya Ofisi za Wakala wa Madini, Dar es Salaam.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kunatokana na taarifa ambazo jeshi hilo lilizipata Juni 29, Mwaka huu kutoka kwa Ally Sadick (40) ambaye ni Ofisa Madini Mkoa wa Dar es Salaam baada ya kugundua kuibiwa madini hayo.Amesema baada ya Polisi kupata taarifa hizo ilianza uchunguzi mara moja na kubaini kuwa madini hayo yaliibiwa na mtuhumiwa huyo kuanzia Desemba, mwaka jana hadi ilipokuja kubainika hivi karibuni.“Baada ya mtuhumiwa kuhojiwa alikiri kuiba madini hayo kidogo ambayo yalikuwa yamehifadhiwa kwenye chumba katika jengo la ofisi za tume ya madini zilizopo Masaki na kueleza kuwa alikuwa akiyauza katika duka la kuuzia vito vya dhahabu,” alisema Mambosasa.Aidha, alisema mtuhumiwa huyo pamoja na kufanya wizi huo, pia alibuni mbinu nyingine ya kuhifadhi madini bandia yenye uzito wa kilo 6.001 nyuma ya jengo la tume ya madini ili kuyapeleka katika chumba walichoiba madini hayo halisi ili kuyabadilisha na yaliyoibiwa kwa lengo la kupoteza ushahidi.Alisema madini hayo halisi ya dhahabu yalikamatwa mwaka 2017 huko maeneo ya bandarini Zanzibar yakiwa yanasafirishwa kinyume cha sheria kisha kuitafishwa na serikali na kuhifadhiwa katika ofisi hizo za tume ya madini.Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linakamilisha utaratibu wa kupeleka jalada kwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali ili mtuhumiwa aweze kufikishwa mahakamani.Aidha, katika hatua nyingine jeshi hilo linawashikilia watu saba kwa tuhuma za wizi wa bajaji mbili, fedha pamoja na bidhaa mbalimbali walioufanya katika maeneo ya Ukonga.Watuhumiwa wanaoshikiliwa ni pamoja na Said Salum (27), Amo Kefas (30), Said Ahmad (38), Mohamed Musa (31), Mboke Samwel (26), Abdallah Kipaneli (25) na Mfaume Mussa (25).Alisema watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo saa nne usiku wa Julai 9 mwaka huu katika maeneo ya Kibeberu na Magole, Ukonga baada ya kuvunja maduka matatu na kufanikiwa kuiba mali hizo.Amezitaja bajaji hizo na namba zake za usajili kuwa ni MC 312 CFB na MC 540 CED zote zikiwa aina ya TVS zenye na rangi ya bluu na kwamba taarifa za wizi huo zilipokelewa katika kituo cha Polisi Stakishari na upelelezi ulianza mara moja ambapo siku hiyo hiyo saa 5 asubuhi watuhumiwa waliweza kukamatwa huko maeneo ya Hondogo Gogoni Kiluvya wilaya ya Ubungo.Aidha watuhumiwa hawa wamekuwa wakifanya matukio ya uhalifu kwa kutumia gari aina ya Toyota Harrier nyeusi yenye namba T.666 DJG ambayo inashikiliwa na Jeshi la Polisi ili kubaini mmiliki wake na kudai kuwa wote watafikishwa mahakamani hivi karibuni.
3
Kulwa Mzee – Dar es Salaam MWANAFUNZI wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Lumola Kahumbi (30), amedai askari wa Kituo cha Polisi Oysterbay alichukua hela zake Sh 12,500, mwingine akamwambia ajiongeze naye akatoweka akiwa njiani kuelekea chooni alikokuwa anapelekwa. Shahidi huyo wa utetezi amedai alikuwa chini ya ulinzi kituoni hapo, akaomba kwenda chooni, akiwa huko askari mmoja akamwambia jiongeze huku mwingine akizamisha mkono mfukoni kwake na kutoka na kiasi hicho cha fedha akabakiwa na Sh 200. Shahidi huyo wa 13 wa upande wa utetezi alidai hao jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba Alidai alikamatwa na askari eneo la Kinondoni Studio na kupelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay Februari 16 mwaka 2018, mfukoni alikuwa na Sh 12,700. “Tuliambiwa kama kuna mtu anataka kujisaidia aseme, mimi nikataka kwenda, nilisindikizwa na polisi wawili,  kabla hatujafika chooni chini ya mwembe askari mmoja akaniambia  jiongeze, mwingine akanisachi na kuchukula Sh 12,500 kisha akaniambia niondoke na nisigeuke nyuma.  “Februari 16,2018 nilitoka chuo na kupanda daladala la Kariakoo/ Makumbusho kwenda Kinondoni Studio kumuona shangazi yangu saa moja na nusu usiku, niliposhuka studio nilielekea nyumba ya nne kwa shangazi,”alidai. Alidai akiwa kwenye daladala aliona magari ya polisi na yalipofika usawa wa kituo cha daladala cha studio, waliruka kutoka kwenye gari zao wakati huo katika barabara hiyo ya Kawawa wananchi walikuwa wakiendelea na shughuli zao na kwamba ule msafara wa gari za polisi ulileta taharuki. Shahidi huyo wa utetezi alibainisha kuwa katika kituo cha daladala cha studio wakati wa tukio hilo kulikuwepo na gari za daladala tatu zikipakia abiria na kondakta wa gari moja wapo alikamatwa. Alidai askari walipoanza kukimbiza watu na kuwakamata alikimbia kuelekea Magomeni lakini alipofika eneo la wauza vitanda askari walimkamata. Wengine walikamatwa wauza viwanda na wateja wao na walikimbia baada ya polisi kuonesha kama kuna kitu wanafanya wananchi wakataharuki na kuanza kukimbia. Alidai kwamba walikamatwa watu wengi na gari nyingi za polisi zilijaza watu ambapo walipofika katika Kituo cha Polisi Osterbay wote waliwekwa eneo la nje ya geti chini ya mwembe na wengine waliwekwa ndani ya geti. Alidai geti lilipofunguliwa walipata wasaa wa kuonana kwa muda wa nusu saa na wakiwa hapo askari waliwapiga kwa kutumia mikanda. Shahidi alidai mmoja kati ya askari hao alitoka ndani ya kituo hicho cha polisi akiwa na ngoma akampa mmoja wao aipige na kuwalazimisha waimbe wimbo wenye maneno ‘dola si lelemama’. Kahumbi alidai ndani ya dakika 20 kuna askari aliwaambia wanaotaka kakwenda chooni wajitokeze na yeye alikuwa miongoni kwa waliojitokeza kutaka kwenda chooni. Wakati akielekea chooni walipofika eneo la chini ya mwembe askari ndipo akanyang’anywa hela aliyokuwa nayo akabaki na Sh 200. Alidai kwa kuwa Sh 200 nilikuwa haitoshi nauli, aliondoka kwa miguu kutoka kituo cha polisi Osterbay hadi DIT. Baada ya ushahidi huyo kueleza hayo, Wakili wa Serikali Salim Msemo, alimuuliza awali kuwa ni kweli mwanachama wa chama cha siasa na asiye mwanachama wanatofautishwa kwa kadi na hizo kadi zina namba na akajibu ni sahihi. Alidai  hakuna uthibitisho wowote ambao ameutoa mahakamani kuthibitisha ni mwanachama wa CCM kama anavyodai katika ushahidi wake. Shahidi wa 14 Shabani Othman anaendelea kutoa ushahidi ambapo alidai alikuwa wakala wa Chadema katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni na baada ya kuapa hakupewa kiapo  hadi Februari 17 asubuhi siku ya uchaguzi. Mbowe na wenzake nane wanashtakiwa kwa mashtaka 13 yakiwemo ya uchochezi na kufanya maandamano haramu Februari 16 mwaka huu.
3
NA MWAMVITA MTANDA YANGA imezindua kwa kishindo tamasha lake lililopewa jina la Wiki ya Wananchi, ambapo wapenzi, wanachama na mashabiki wa klabu hiyo nchi nzima watafanya shughuli za kijamii. Tamasha hilo lililozinduliwa jana Dar es Salaam, litafikia tamati Agosti 4, Uwanja wa Taifa jijini humo, ambapo kikosi cha timu hiyo kitakachoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao na mashindano mengine, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika kitatambulishwa. Mbali ya kutambulisha wachezaji, timu hiyo itashuka dimbani kuumana na Kariobangi Sharks ya Ligi Kuu ya Kenya, katika mchezo  wa kirafiki  utakaopigwa kwenye uwanja huo. Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Wiki ya Wananchi, Rogers Gumbo alisema, lengo la kunzisha tukio hilo kuwakutananisha wanachama wa Yanga na kufanya shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo kufanya usafi na kutembelea wagojwa katika hospitali. “Hii wiki ni muhimu sana kwetu tena ya kihistoria tangu kuanzishwa kwa klabu hii, hivyo naweza kusema itasaidia kuwajenga Wanayanga na kutambua majukumu yao katika jamii,”alisema Gumbo. Rogers alisema  baadhi ya wanachama wa klabu hiyo leo watasafiri kwenda Zanzibar ambako watakutana na wadau na mashabiki wa huko na kufanya mkutano mkubwa wa wanachama. Alisema wakiwa huko, watawatembelea wagonjwa na kufanya usafi katika maeneo mbalimbali. Alisema Wiki ya Wananchi itaenda sambamba na burudani za ngoma za asili.
4
SERIKALI kupitia Kampuni ya Huduma za Meli Tanzania (MSCL) kwa kushirikiana na Shirika la Reli Uganda wameweka utaratibu wa kuwa na kituo kimoja cha malipo ya mizigo inayosafirishwa kutoka Dar es Salaam kwenda Bandari ya Mwanza hadi Port Bell nchini Uganda, ili kuboresha huduma za usafirishaji wa mizigo na abiria kwa nchi hizo mbili.Hiyo ni katika kurahisisha biashara ya usafirishaji wa mizigo, ikiwamo kupunguza gharama za usafirishaji kwa wafanyabiashara na wawekezaji wanaotumia huduma za usafirishaji kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC). Hayo yamesemwa jana jijini hapa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe alipozungumza katika hafla maalumu ya tukio la kihistoria ya uzinduzi wa huduma ya usafirishaji wa mizigo na abiria katika ushoroba wa kati kwa njia maji kupitia Ziwa Victoria kwenda bandari ya Port Bell, Uganda.Kamwelwe alisema mizigo itakuwa inasafirishwa kwa reli kutoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda Mwanza na baadaye itasafirishwa kwa kutumia meli ya mizigo ya Mv Umoja kwenda Uganda na nchi jirani za Maziwa Makuu, kwa lengo la kuhudumia wananchi na nchi hizo zinazotumia bandari nchini kusafirisha mizigo na abiria. Waziri alifanya uzinduzi huo katika Bandari ya Mwanza Kusini katika hafla maalumu ya tukio la kihistoria ya kuanza kwa safari ya meli ya mizigo ya Mv Umoja itakayosafirisha mizigo kutoka Mwanza kwenda Uganda.Kamwelwe alisema treni ya mizigo itakapokuwa inawasili katika Bandari ya Mwanza itaingia moja kwa moja kwenye meli ya mizigo bila kushusha mzigo na kwenda nchini Uganda. “Ni jambo la kujivunia kwani ni nchi chache katika Afrika zenye miundombinu iliyounganishwa kwa utaratibu huu,” alisema na kuongeza kuwa utaratibu huo wa muunganiko wa njia za reli na maji katika usafirishaji wa mizigo na abiria, utawezesha mzigo unaposhuka kwenye meli katika Bandari ya Dar es Salaam kupakiwa kwenye treni ya TRC na kusafirishwa moja kwa moja kwenda jijini Mwanza.“Mfumo huu wa usafirishaji upo pia upande wa nchi jirani ya Uganda ambapo huwezeshwa mzigo kufika Kampala bila kushushwa kwenye treni,” alisema. Alibainisha kuwa taarifa zilizopo zinaonesha kuwa tangu kufunguliwa kwa njia hiyo ya usafirishaji Juni 6, 2018, jumla ya mabehewa 1,165 sawa na tani 45,720 zimekwishasafirishwa kupitia ushoroba huo kwa njia ya reli na maji. Alisema kati ya mzigo huo, mabehewa 864 sawa na tani 34,960 yalikuwa yamesafirisha mzigo wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) ambalo lilichangia takribani asilimia 75 ya mzigo wote uliosafirishwa katika kipindi hicho. Naye Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema kukamilika kwa huduma hiyo ya usafiri katika ushoroba wa kati ni kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi ambao utatoa fursa kwa nchi kutengeneza uchumi wa viwanda utakaoangalia masoko ya nje.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alisema usafirishaji huo wa njia ya reli na majini kwenda nchini Uganda utaboresha shughuli za kiuchumi kwa Jiji na Mkoa wa Mwanza na Taifa kwa ujumla. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkazi wa WFP, Michael Dunford aliishukuru serikali kwa jinsi ambavyo katika kipindi cha mwaka mmoja meli ya Mv Umoja ilisafirisha kontena 18 za mizigo zenye chakula cha msaada uliotolewa na WFP kwenda nchini Uganda.
3
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi imewahukumu vigogo wa Kampuni ya Vodacom Tanzania PLC na Kampuni ya Inventure Mobile Tanzania Limited T/A Tala Tanzania, kulipa faini ya zaidi ya Sh bilioni 6.012, waliyoisababisha kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).Katika faini hiyo, Sh milioni 120 ni faini ya mashitaka saba yanayowakabili washitakiwa wote au kwenda jela miaka saba, endapo watashindwa kulipa faini. Washitakiwa katika kesi hiyo ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Vodacom, Hisham Hendi raia wa Misri, Mkuu wa Kitengo cha Mapato wa Vodacom PLC, Joseph Nderitu raia wa Kenya, Mkurugenzi wa Sheria, Olaf Mumburi mkazi wa Victoria Kinondoni, Mkuu wa Kitengo cha Mauzo wa kampuni hiyo, Joseph Muhere, Meneja wa Uhasibu, Ibrahim Bonzo na Kampuni ya Vodacom iliyopo Ursino Estate Barabara ya Bagamoyo.Washitakiwa wa Kampuni ya Tala ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari ambaye ni raia wa Kenya, Brian Lusiola, Meneja Uendeshaji wa Biashara wa Kampuni ya Inventure Mob Tz Ltd, Ahmed Ngassa na Kampuni ya Inventure Mobile Tanzania Limited T/A Tala Tanzania. Akisoma adhabu hiyo jana baada ya washitakiwa kukiri makosa yao, Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alisema kuwa kuanzia mashitaka ya kwanza hadi ya sita, washitakiwa ambao ni Lusiola, Ngassa na Kampuni ya Tala, watatakiwa kulipa faini ya Sh milioni tano kwa kila mashitaka au kifungo cha jela mwaka mmoja ambayo ni sawa na Sh milioni 90 kwa pamoja.Katika mashitaka ya kuisababishia TCRA hasara ya Sh milioni 642.2, mahakama hiyo imeamuru washitakiwa Lusiola, Ngassa na Kampuni ya Tala, kulipa hasara hiyo na endapo watashindwa, watarudishwa mahakamani na kupangiwa adhabu. Kwa upande wa Kampuni ya Vodacom, ambao wanakabiliwa na mashitaka mawili ya kuruhusu matumizi ya namba zinazotolewa na TCRA na kusababisha hasara ya Sh 5,250,237,000, wametakiwa kulipa kila mmoja faini ya Sh milioni tano, ambayo jumla ni Sh milioni 30 na kulipa hasara hiyo yote.“Mahakama inataifisha vifaa vyote vya kieletroniki vilivyotumika kwenye kughushi namba hizi na kusababisha kuingia kwa mawasiliano ya kimataifa ambayo yangeweza kusababisha hatari kwenye masuala ya ulinzi na usalama wa nchi,” alisema Hakimu Shaidi. Akisoma maelezo ya awali namna udanganyifu huo ulivyofanywa, Wakili wa Serikali, Jacqueline Nyantori akisaidiana na Simon Wankyo, alidai kuwa Kampuni hiyo ya Tala ambayo imesajiliwa nchini iliingia mkataba na Kampuni ya Vodacom wa kulipwa Sh milioni tisa ili kupata namba hizo ambazo mwenye mamlaka ya kuzitoa ni TCRA. Alidai mkataba huo ulikuwa kinyume na sheria, na kwamba Vodacom iliruhusu kufanyika kwa makosa hayo ya kughushi namba.Kabla ya kutolewa adhabu hiyo, Wakili Nyantori alidai kuwa hawana rekodi ya makosa ya nyuma ya washitakiwa hao na kwamba kutokana na asili ya makosa yaliyofanywa na washitakiwa, kutumika kwa namba zilizoghushiwa, ingechangia kuruhusu simu za Kimataifa kusambazwa nchini na isingeweza kuthibitiwa kama ilivyo kwa laini. Alidai tangu kuingia kwa mawasiliano hayo ya kimataifa, serikali ya Tanzania haikuwa inatambua ni kitu gani kinachoingia kutoka nje ya nchi hivyo kusababisha hatari kwa usalama wa nchi.“Tunaomba Mahakama itoe adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwao na watu wengine ambao wanatarajia kufanya makosa kama hayo. Pia tunaomba kutaifisha vifaa vilivyotumika kufanya makosa haya na Mahakama itoe amri kuhusu hasara iliyosababishwa,” alidai Nyantori. Wakili wa Utetezi, Seni Malim aliiomba mahakama kuwapunguzia adhabu washitakiwa ikiwemo Vodacom, kwa sababu ni wakosaji wa kwanza na kwamba ni walipa kodi wakubwa na wametoa ajira kwa Watanzania wengi.Alidai mshitakiwa Hendi ameajiriwa katika kampuni hiyo hivi karibuni, hivyo alikuta tayari makosa yamefanywa na wafanyakazi wengine, na Mumburi alichaguliwa katika Kitengo cha Sheria cha kampuni hiyo mwezi mmoja uliopita. Katika mashitaka yao, inadaiwa Lusiola, Ngassa na Kampuni ya Tala, kati ya Januari Mosi na Desemba 31, mwaka jana, maeneo ya jengo la Tanzania Park lililopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, kinyume na sheria waliingiza vifaa vya kieletroniki bila kuwa na leseni cha TCRA.Pia inadaiwa mwaka jana katika maeneo hayo, Lusiola, Ngassa na Kampuni ya Tala, walisimika na kutengeneza vifaa vya kieletroniki vya mawasiliano bila kuwa na leseni inayotolewa na TCRA. Nyantori alidai kuwa washitakiwa hao kati ya Aprili 17, mwaka jana na Machi 11, mwaka huu maeneo hayo, waliendesha mitambo hiyo bila kwa kupokea na kusambaza upokeaji wa simu za kimataifa bila kuwa na leseni hiyo.Katika mashitaka ya tano, inadaiwa kutoka Aprili 17, mwaka jana na Machi 11, mwaka huu maeneo hayo, walikwepa kodi ya kupokea na kusambaza huduma ya upokeaji wa simu za kimataifa kwa kusambaza mawasiliano kwa kutumia mfumo huo. Washitakiwa hao pia wanadaiwa kutoka Aprili 17, mwaka jana na Machi 11, mwaka huu maeneo hayo, kinyume na sheria walitumia vifaa vya mawasiliano kuunganisha huduma ya kielektroniki ya mawasiliano kwa lengo la kupokea na kusambaza mfumo wa mawasiliano bila kupata kibali cha TCRA.Inadaiwa katika tarehe hizo, maeneo hayo, Ngassa, Lusiola na Kampuni ya Tala, walitumia namba 813 za Vodacom ambazo ni namba maalumu bila kupewa na TCRA. Katika mashitaka ya tisa, Wakili Wankyo Simon alidai kuwa Hendi, Nderitu, Mumburi, Muhere, Bonzo na Kampuni ya Vodacom, kati ya Aprili 17, mwaka jana na Machi 11, mwaka huu maeneo ya jengo la Vodacom lililopo Ursino Estate Barabara ya Bagamoyo, Dar es Salaam, waliwaruhusu Ngassa, Lusiola na Tala kutumia namba 813 za Vodacom bila kuzipata kutoka TCRA.
3
Na Dennis Luambano, Dar es Salaam RAIS mteule wa Marekani, Donald Trump, ametoa mwelekeo wa namna atakavyoiendesha nchi hiyo ndani ya siku 100 za kwanza za utawala wake. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la CCN, mwelekeo huo alioutoa New York juzi, umeashiria namna atakavyolegeza baadhi ya misimamo yake, ukiwamo wa kufutilia mbali Mkataba wa Paris, unaohusu mabadiliko ya tabianchi, tofauti na alivyoahidi wakati wa kampeni za urais kabla hajachaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo, Novemba 8, mwaka huu. Licha ya kulegeza msimamo wake katika baadhi ya mambo, lakini ahadi yake ya kuwashughulikia magaidi wa Dola ya Kiislamu (IS) iko palepale. Ndiyo, kama alivyoahidi wakati wa kampeni zake kwamba yeye ndiye mwenye msuli na stamina ya kuwatwanga mabomu IS kuliko aliyekuwa mpinzani wake wakati wa uchaguzi huo, Hillary Clinton. Kwamba anaamini njia pekee ya kuwatokomeza IS ni kuwapiga kwa mabomu na anasisitiza kuwa hakuna mwingine mwenye uwezo wa kuchukua uamuzi mzito kama huo zaidi yake. Pia atawadhoofisha IS kwa kulipua vyanzo vyao vya mafuta. Wakati akiwa na msimamo huo kuhusu IS, lakini anasema dunia ingekuwa bora kama aliyekuwa Rais wa Irak, Saddam Hussein na aliyekuwa Kiongozi wa Libya, Kanali Mummar Gaddafi, wangekuwa madarakani. Trump anaamini kuwa ili kutatua matatizo yanayoikabili dunia sasa hivi ingekuwa jambo jema zaidi kama Saddam na Gaddafi wangelikuwapo madarakani. Kimsingi, imani hiyo ya Trump inakinzana na watangulizi wake, Rais Barrack Obama aliyeruhusu majeshi kumng’oa Gadaffi na Rais Mstaafu George W. Bush, aliyeruhusu majeshi hayo hayo kumng’oa Saddam, hasa ikizingatiwa kuwa sasa hivi ngome kuu za IS ziko Irak na Libya, huku kila siku wakiendelea kufanya mashambulizi katika nchi za Mashariki ya Kati, ikiwamo Syria. Pamoja na msimamo wake kukinzana na watangulizi wake, lakini pengine Trump anajifanya hajui mizizi ya dubwana la IS, kwamba ni kama mradi wa nchi hiyo kwa kushirikiana na kampuni kubwa za kigeni za kutengeneza silaha za kivita. Kwamba IS imeumbwa ili eneo la Mashariki ya Kati lionekane ni hatari kwa Serikali zilizopo madarakani katika maeneo hayo na kwa kuwa kuna utajiri mkubwa wa mafuta, ina maana biashara ya silaha za kukabiliana nao itaendelea kufanyika. Kama hivyo ndivyo, ina maana ule msimamo wake kwamba atazifurumusha kampuni zinazoinyonya Marekani kutokana na migogoro ya Mashariki ya Kati ni kama vile hatafanikiwa kuusimamia, kwa sababu kitendo cha kutaka kuiangamiza IS ndivyo kampuni hizo zitakavyoendelea kujinufaisha. Kwa sababu kampuni kubwa za kuuza silaha nyingi kati ya hizo zikiwa za Wamarekani na Wazeyuni zitawafadhili au zitawauzia silaha kwa pande zote mbili, kwa maana ya IS na Serikali zinazokabiliana nao. Kwa hiyo wanachokifanya IS na kinachoendelea Mashariki ya Kati ni zaidi ya ugaidi, kwa sababu kuna biashara kubwa ya kubadilisha mafuta kwa silaha. Ndiyo! Licha ya watu kupoteza maisha kutokana na matendo ya IS, lakini nyuma ya pazia ni kwamba ugaidi wao ni wa ‘kiwango cha lami’, kwa maana umeboreshwa na biashara inayofanyika, hasa kwa kuzingatia kuwa ugaidi si imani moja kwa moja kama ukilinganisha matukio mengine ya kigaidi yaliyotokea siku za nyuma katika maeneo mbalimbali. Mathalani, kitendo cha majeshi washirika yakiongozwa na Marekani kuivamia Irak mwaka 2001 na kuupiga utawala wa Saddam kisha wakamnyonga Desemba, 2006, nao ni ugaidi uliohalalishwa. Pia kitendo cha majeshi hayo hayo cha kuivamia Libya kisha Oktoba, 2011 wakamuua Gaddafi nao ni ugaidi. Kwa sababu licha ya kuwaua viongozi hao kwa visingizio vya kipuuzi ambavyo hadi leo havijathibitishwa, mathalani Saddam walisema ana silaha za maangamizi ya halaiki, Gaddafi walidai ni dikteta anayeminya demokrasia nchini mwake, waliharibu mali na miundombinu, huku kampuni za nchi washirika zikazawadiwa kandarasi za kuzijenga upya kwa malipo ya kunyonya malighafi ya mafuta yanayopatikana kwa wingi katika nchi hizo. Kwa hiyo wakati Trump akishikilia msimamo wake wa kuiangamiza IS, anapaswa kufahamu namna nchi yake inavyonufaika na migogoro ya Mashariki ya Kati kama nilivyotoa mfano wa Libya na Irak, kwamba si ugaidi tu kama dunia inavyoaminishwa, bali kuna biashara kubwa inafanyika nyuma ya pazia. Pia, si biashara tu, bali Marekani inajiingiza katika migogoro ya namna hiyo tangu enzi na enzi ili kulinda masilahi yake katika majukwaa ya kimataifa. Kuthibitisha hoja yangu, tutafakari uchambuzi wa Aubrey Bailey aliowahi kuutoa mwaka jana, akisema kinachotokea katika nchi za Mashariki ya Kati kisiishangaze dunia, kwa sababu Marekani inaisaidia Irak katika vita ya kuwaondoa IS. Kwamba Marekani hiyo hiyo haiipendi IS, lakini inaupenda utawala wa Saudi Arabia unaoipenda IS. Pia haimpendi Rais wa Syria, Bashar Assad na wanafurahia mapigano yanayotaka kumng’oa madarakani yanayofanywa na IS, ingawa hawaipendi. Alisema Marekani haiupendi utawala wa Iran, ingawaje unaisaidia Irak kuwaangamiza IS. Tafsiri ya uchambuzi wa Bailey ni kwamba, baadhi ya marafiki wa Marekani wanawaunga mkono maadui zake, baadhi ya maadui zake ni marafiki zao kwa namna moja au nyingine, kwa kuwa baadhi yao wanapigana na maadui zake wengine. Aidha, hawataki maadui zake wawapige maadui zake wengine kwa sababu wakishinda watakuwa maadui hatari zaidi kwa Marekani kwa kuwa ilijiingiza katika vita ya kupambana na ugaidi katika nchi ambazo awali hazikuwa na magaidi, bali ilipoingia tu ndipo ugaidi nao ukaibuka.
2
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri, Abdel Fattah Al-Sisi, ambapo wametumia fursa hiyo kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi zote mbili kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo uchumi.Mbali na kuzungumzia masuala hayo ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kisiasa, kiuchumi na kijamii, pia Waziri Mkuu amemfikishia Rais wa Misri salamu kutoka kwa Rais wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli.Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, mazungumzo baina ya Waziri Mkuu na Rais wa Misri yaliyofanyika jana Ikulu jijini Cairo, ikiwa ni katika siku ya tatu na ya mwisho ya ziara yake ya kikazi nchini Misri.Waziri Mkuu aliambatana na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga alimaliza ziara yake ya kikazi nchini Misri ambapo aliagwa na Waziri wa Kilimo na Uhaulishaji wa Ardhi wa Misri, Dk Ezz Eldien Abo Setit katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Cairo.Akiwa ziarani nchini Misri, Waziri Mkuu alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Misri, Dk Mostafa Madbouly katika siku yake ya kwanza ya ziara yake, ambapo aliwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Misri waje kuwekeza nchini.Pia, Waziri Mkuu alitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo nchini humo ambayo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa makao makuu mapya ya nchi hiyo, mradi wa awamu ya pili ya upanuzi wa mfereji wa Suez na kiwanda kikubwa cha ngozi.
3
MADRID, HISPANIA KOCHA mpya wa timu ya taifa ya Hispania, Luis Enrique, ameahidi kufanya mambo makubwa, ikiwamo kukisuka upya kikosi cha kwanza cha timu hiyo. Enrique, ambaye alikuwa kocha wa Barcelona, amechukua mikoba ya aliyekuwa kocha wa Hispania, Fernando Hierro, ambaye alifukuzwa baada ya kufanya vibaya katika michuano ya Kombe la Dunia iliyomalizika nchini Urusi. Hierro alikuwa kocha wa muda baada ya kocha aliyefanikiwa kuivusha timu hiyo kufuzu michuano ya Kombe la Dunia, Julen Lopetegui, kufukuzwa siku chache baada ya kukubali kujiunga na klabu ya Real Madrid. Katika michuano hiyo nchini Urusi, Hispania ilishinda mchezo mmoja wa makundi dhidi ya Iran na baadaye kuondolewa na Urusi katika hatua ya 16 bora. “Hayatakuwa mapinduzi, haya ni mageuzi. Kwani unaweza kubadilisha mtindo wa kucheza bila kubadilisha kitu kingine, kama nilivyoonyesha nikiwa Barcelona. “Soka ni mageuzi endelevu na tuna wazo la kufanya hivyo. Tunaweza kucheza soka nzuri, kuwa na nguvu, kudhibiti mpira na kuwaumiza wapinzani wetu.Kuna vitu tunahitaji kuboresha, pia,” alisema Enrique. Enrique, ambaye aliwahi kuwa kocha wa Barcelona kati ya mwaka 2014 na 2017 na kushinda mataji mawili, likiwamo Ligi Kuu ya Hispania na Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2015, pia aliongeza kuwa, atachagua wachezaji  wenye viwango na aina ya uchezaji wao, lakini si wenye majina makubwa. “Naona kama nachelewa kutangaza kikosi changu cha kwanza, kitawashangaza wengi, nina uhakika, kikosi cha awamu ya kwanza kitakuwa na wachezaji kama 70. “Wachezaji wengi miongoni mwao hawatakuwa na uhakika wa kucheza kikosi cha kwanza na sitazungumza na mchezaji yeyote,” alisema. Miongoni mwa kazi yake ya kwanza kocha huyo itakuwa kumshawishi beki Gerard Pique kuacha mpango wake wa kustaafu soka la kimataifa, baada ya kuahidi kufanya hivyo wakati michuano ya Kombe la Dunia itakapomalizika. “Pique ni shughuli maalumu, kwani miaka miwili iliyopita alitangaza kujiuzulu. Napenda kuwa na wachezaji wote, akiwamo beki huyo, ameonyesha kuwa na kiwango kizuri, hata hivyo unatakiwa kuheshimu mawazo ya wengine,” alisema.
4
Na TUNU NASSOR-DAR ES SALAAM WATAALAMU 11 kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wamepelekwa katika Hospitali ya Apollo nchini India kwa mafunzo ya vitendo ya mwezi mmoja, ikiwa ni maandalizi ya hospitali hiyo kuanza kutoa huduma ya upandikizaji wa uloto mwishoni mwa mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba MNH, Dk. Hedwiga Swai, alisema wataalamu hao ni pamoja na madaktari bingwa wa magonjwa ya damu watatu, wataalamu wa maabara watatu na wahandisi watatu. Wengine ni mtaalamu wa fedha atakayefanya uchambuzi wa gharama za huduma hiyo pamoja na mtaalamu wa manunuzi atakayechambua dawa na vitendanishi vinavyotumika na upatikanaji wake. Alisema kundi jingine la wauguzi watatu, wataalamu wa saratani ya watoto watatu, mfamasia mmoja na wataalamu wengine wawili, walikwishapata mafunzo ya miezi mitatu ya jinsi ya kutoa huduma hiyo. “Gharama zilizotumika kuwapeleka wataalamu hao katika mafunzo hayo ni Sh milioni 91 zikijumuisha gharama za mafunzo, nauli, fedha za kujikimu na gharama nyingine ambapo fedha hizo zimetolewa na MNH,” alisema Dk. Swai. Alisema matibabu hayo kwa nje ya nchi inakadiriwa kugharimu Sh milioni 200 kwa mgonjwa mmoja anayepandikizwa uloto kutoka kwa ndugu yake na Sh milioni 150 kwa anayepandikizwa uloto wake mwenyewe. Akizungumzia maandalizi ya miundombinu, Dk. Swai alisema Serikali imetoa Sh bilioni 6.2 ambapo kati yake Sh bilioni 3.7 zimetumika kwa maandalizi ya ununuzi wa vifaa na kuweka miundombinu ya kutolea huduma hiyo. Aliongeza kuwa takwimu za MNH zinaonesha kuwa wagonjwa kati ya 130 na 140 huhitaji huduma hiyo kila mwaka ambapo zaidi ya theluthi mbili ya wagonjwa hupoteza maisha kwa kukosa huduma hiyo. “Uwepo wa huduma hii utasaidia wananchi wengi kutibiwa hapa nchini, kujenga uwezo kwa wataalamu wa ndani, itapunguza mzigo kwa Serikali kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwani gharama za kupata huduma hii zitashuka kwa asilimia 50 kwa mgonjwa mmoja,” alisema. Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa ya Damu MNH, Dk. Stella Rwezaura, alisema huduma ya upandikizaji wa uloto hutolewa kwa kupandikiza chembechembe mama za kuzalisha damu ambazo hupatikana kwenye uloto  au zile zinazotoka kwenye kitovu cha mtoto au kondo la nyuma la mama. Aliongeza kuwa upandikizaji huo huanza kwa kumwandaa mgonjwa ambaye chembechembe zake za damu zina tatizo kama saratani ya damu, selimundo na wale ambao mifupa yao inashindwa kuzalisha damu. “Hii hufanyika kwa kuwapa tiba maalumu ya kuziua chembechembe zote zenye matatizo kisha kupandikiza mpya zilizopo kwenye uloto kutoka kwa ndugu yake mwenye vinasaba vinavyofanana au zilizozalishwa kutoka kwa mgonjwa mwenyewe,” alisema Dk. Stella. Alisema kuwa tiba hiyo ndiyo pekee inayoweza kumtibu na kumponya mgonjwa mwenye matatizo hayo. Tanzania itakuwa nchi ya kwanza kupandikiza uloto katika ukanda wa Afrika Mashariki na ya sita katika Bara la Afrika. Kwa sasa huduma hii Afrika inatolewa Afrika Kusini, Tunisia, Misri, Comoro na Nigeria.
0
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji, ameipa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Dar es Salaam miezi miwili na nusu hadi ifi kapo Desemba 31 mwaka huu, kuandaa na kuwasilisha wizarani orodha ya walipakodi, idadi ya majengo na mabango yote yaliyoko katika mkoa huo ili kupata takwimu sahihi za idadi ya walipakodi.Dk. Kijaji alisema hayo jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kikazi TRA Mkoa wa Kikodi wa Temeke ili kukagua utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hayo, kubaini fursa na changamoto za masuala ya ukusanyaji kodi.Alisema pamoja na mamlaka hiyo kufanya vizuri katika makusanyo ya mapato ya Septemba 2019, ambapo Sh trilioni 1.78 zilikusanywa, kiasi hicho bado ni kidogo, ikilinganishwa na mwamko wa wananchi uliopo hivi sasa katika kulipa kodi.Aliitaka TRA kuwasilisha kwake takwimu ya ongezeko la walipa kodi, lililotokana na zoezi la kugawa vitambulisho vya wajasiriamali nchini, kwa kuwa lengo la Rais John Magufuli kugawa vitambulisho ni kuongeza kuongeza wigo wa walipa kodi, kujua idadi yao kamili na mahali walipo.Kwa upande wa kodi ya majengo, Dk. Kijaji aliitaka TRA kuhakikisha inapata orodha ya nyumba zote nchini kwa kuorodhesha wamiliki wa nyumba hizo, mawasiliano yao na kisha kuandaa kanzidata, itakayorahisisha ukusanyaji wa kodi hiyo.“Ili kuongeza mapato yanayotokana na kodi ya majengo ni lazima TRA wafanye kazi usiku na mchana kuhakikisha kanzidata hiyo inakamilika, ambayo itatumika kuwakumbusha walipa kodi kupitia ujumbe mfupi wa simu. Itasaidia ukusanyaji wa kodi hiyo kama ilivyo kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inapowakumbusha wananchi kulipa kodi ya ardhi kupitia simu zao,”alisema.Aliongeza “Nataka pia mkague watumiaji wote wa mashine za utoaji risiti za kieletroniki (EFD) kwa wafanyabiashara wa Temeke ili kuhakikisha kila anayeuza anatoa risiti na anayenunua anadai risiti na kwa kufanya hivyo itasaidia kuongeza makusanyo ili taifa liendelee kujitegemea kimapato” .Awali, akimkaribisha Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Kikodi wa Temeke, Paul Walalaze, alisema mkoa wake una idadi ya walipakodi 437,539.Alisema mwaka 2018/19 mkoa wake ulipanga kukusanya Sh bilioni 395 na ulifanikiwa kukusanya Sh bilioni 328.5, sawa na asilimia 85 ya lengo.“Tumekusanya pia kodi ya majengo shilingi bilioni 1.4 kati ya malengo ya kukusanya shilingi bilioni 1.6, kodi ya mabango shilingi bilioni 2.2 kati ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 2.3 sawa na mafanikio ya asilimia kati ya 87 na asilimia 95,”alisema.Ofisa Mwandamizi Mkuu wa TRA, Hamisi Lupenja, alimhakikishia Dk. Kijaji kwamba watatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa ili kuboresha ukusanyaji wa mapato ya serikali, ikiwemo kutoa elimu kwa walipakodi.
5
WASHITAKIWA walioandika barua kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kukiri makosa ya uhujumu uchumi yanayowakabili, kufuatia msamaha uliotolewa na Rais John Magufuli, wanazidi kujitokeza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.Miongoni mwa washitakiwa waliokiri na kuadhibiwa kulipa faini jana katika mahakama hiyo ni Mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) na Polisi watano, ambao wametakiwa kulipa faini ya Sh milioni 7.6 au kutumikia kifungo cha miaka saba jela, baada ya kukiri kuiba mafuta ya ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).Mwingine ni raia wa Vietnam, Bui Nhi ambaye amehukumiwa kulipa faini ya zaidi ya Sh milioni 22, baada ya kutiwa hatiani katika mashitaka ya kujihusisha na nyara za serikali bila kibali.Hata hivyo, washitakiwa wengine ambao wanataka kukiri makosa yao ikiwemo aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Michael Wambura na watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), akiwemo Mkurugenzi Mtendaji, Dickson Maimu na wenzake watafikishwa mahakamani hapo Jumatatu Oktoba 7, mwaka huu kwa ajili ya kuendelea na mchakato wa kukiri makosa yao.Kati ya askari waliohukumiwa ni Koplo Shwahiba (38) MT. 74164 SGT, Ally Chibwana (47) wa JWTZ, Konstebo Elidaima Pallangyo (38), Konstebo Simon (28), Konstebo Dickson na Konstebo Hamza, ambao walifutiwa mashtaka ya utakatishaji fedha na kupanga genge la uhalifu na kubaki na mashitaka ya wizi.Kabla ya kufutiwa mashitaka yao, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Renatus Mkude alidai mbele ya Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo kuwa wameingia makubaliano na washitakiwa hao kumaliza shauri hilo, hivyo anaiomba makubaliano hayo yawe sehemu ya shauri hilo.Hakimu Mwaikambo alisema ni lazima mahakama ijiridhishe, kama ni kweli washitakiwa waliweka makubaliano hayo kwa hiari bila kulazimishwa, ambapo walikiri kwamba waliandika makubaliano wenyewe. Akitoa adhabu, Hakimu Mwaikambo alisema amezingatia kwamba washitakiwa ni wakosaji wa kwanza na kwa kuzingatia msamaha uliotolewa na Rais wa washitakiwa kukiri makosa yao, hivyo kupunguziwa kiwango cha makosa yao.“Adhabu kila mshitakiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi 500,000 kila mmoja au kifungo cha miaka saba jela, pia mtatakiwa kulipa thamani yote mliyosababisha hasara ya shilingi 4,647,760. Pia magaloni yote ya mafuta yanataifishwa na kuwa mali ya serikali,” alisema Hakimu Vick.Wakili Mkude alidai shauri hilo limeingia utaratibu wa makubaliano, hivyo suala la adhabu anaiachia mahakama. Pia aliomba warudishe hasara waliyosababisha na kutaifisha madumu 109 ya mafuta ya ndege.
3
MKAKATI wa Serikali kutafuta masoko ya bidhaa za Tanzania nje unaendelea kuzaa matunda ambapo kwa sasa vitunguu swaumu vimepata soko kwenye nchi tisa. Ilielezwa bungeni jana kuwa vinauzwa vikiwa ghafi.Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba ndiye aliyesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Massay (CCM) aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kutafuta soko la vitunguu swaumu nje ya nchi.“Vitunguu swaumu vinauzwa katika nchi ya Shelisheli, visiwa vya Comoro, Msumbiji, Zambia, Mauritania, Kenya, Uganda na Falme za Kiarabu,” alisema. Mgumba alisema katika kuhakikisha upatikanaji wa masoko ya uhakika kwa mazao ya kilimo vikiwemo vitunguu swaumu, serikali imekamilisha upatikanaji wa simbomilia (barcode)pamoja na kubainisha viwango vya ubora kwa kulitumia Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Aidha, wizara imeanzisha kitengo cha masoko chenye jukumu la kuyatafuta ndani na nje ya nchi ikiwemo ya vitunguu swaumu. Alisema wanayatafuta masoko hayo wakiwa wanajua viwango vya ubora wa bidhaa, bei na muda wa kuhitajika mazao hayo sokoni. Hayo yote yanafanyika ili kuwa na taarifa sahihi za kuwapa wakulima waweze kuzalisha mazao yanayokidhi mahitaji ya soko. Alisema, serikali kupitia Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) ilivijengea uwezo vikundi vya wakulima katika bonde la Bashay na kuviwezesha kusindika vitunguu swaumu.“Jitihada hizo zimesaidia kuongeza thamani ya zao la vitunguu swaumu, muda wa kuvihifadhi bila kuharibika na kuimarisha soko la bidhaa hiyo ndani na nje ya nchi,” alisema.Alisema wakulima na wasindikaji wa vitunguu swaumu wa Mbulu huwezeshwa kushiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam kila mwaka kutangaza na kutafuta masoko ya vitunguu swaumu na bidhaa zake ndani na nje ya nchi. Alisema serikali kwa kushirikiana na asasi isiyo ya serikali ya Global Communities iliandaa kongamano la vitunguu swaumu lililofanyika katika bonde la Bashay Aprili 16, mwaka huu katika AMCOS ya Didihama ambapo wafanyabishara kutoka sehemu mbalimbali za nchi walialikwa kwa lengo la kutafuta soko la vitunguu saumu.
3
Waandishi wetu-Iringa WAZIRI wa Adhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewataka wakurugenzi wa halmashauri kujitathmini katika idadi ya hati za ardhi wanazotoa kwa wamiliki wa ardhi kwenye halmashauri zao. Lukuvi alisema hayo jana katika mkutano wake wa kusikiliza na kutatua kero za ardhi kwa wananchi wa Mkoa wa Iringa kupitia programu ya Funguka kwa Waziri uliofanyika ukumbi wa Siasa ni Kilimo, Manispaa ya Iringa, Alisema wizara yake itaanza kutangaza wilaya itakayoongoza katika upangaji, umilikishaji na utoaji hati za ardhi kwa wananchi ili kubaini ambazo ziko nyuma.  “Mkurugenzi ajione fahari kuwawezesha wananchi kwa kupima na kuwapatia hati, kama mkurugenzi huwezi kutoa hatimiliki hata mia moja basi wewe hufai,” alisema Lukuvi. Alisema kumilikisha na kumpatia mwananchi hati ya ardhi ni kumwezesha kiuchumi kwa kuwa anaweza kuitumia hati kwenye shughuli za kimaendeleo na kusisitiza kuwa wakurugenzi wa halmashauri wahakikishe wanapanga na kuwamilikisha maeneo wananchi. Lukuvi alisema kwa sasa wizara yake imejipanga kuhakikisha inasogeza huduma za ardhi karibu na wananchi kwa kuanzisha ofisi za mikoa zitakazokuwa na watendaji wote wa sekta ya ardhi kama vile wapimaji, wathamini, wataalamu wa mipango miji pamoja na wasajili. “Sasa wapimaji, wathamini na wapangaji watakuja hapa Iringa, muundo unaanza mwezi ujao, lengo ni kuwapunguzia usumbufu wananchi katika kupata huduma za ardhi,’’ alisema Lukuvi. Alisema katika kuboresha huduma za sekta ya ardhi, wizara yake itatumia mifumo unganishi utakaorahisisha utendaji kazi kwa wataalamu wa sekta ya ardhi ambapo kazi kubwa itakuwa ikifanyika kielektroniki badala ya kutumia makaratasi aliyoeleza kuwa wakati mwingine husababisha tamaa kwa maofisa ardhi. Alitolea mfano Mkoa wa Dar es Salaam, umeshaanza kutumia mfumo unganishi ambapo sasa wamiliki wa ardhi wanapatiwa hati za kielektroniki na kubainisha kuwa lengo la kuwa na mfumo unganishi ni kuondoa urasimu na kurahisisha utendaji kazi. Naye Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi alieleza mkoa wake umejitahidi kupunguza kero na migogoro ya ardhi iliyokuwapo miaka ya nyuma kwa kuanzisha utaratibu wa kuwafuata wananchi kwenye maeneo yao kupitia programu ya Iringa Mpya. Alimweleza Lukuvi kama angekuja mwaka mmoja na nusu uliopita, basi ukumbi aliofanyia mkutano wa Funguka kwa Waziri ungekuwa umejaa wananchi wenye kero za ardhi, lakini jitihada za mkoa wake zimesababisha mkutano huo kutokuwa na idadi kubwa ya wananchi wenye migogoro ya ardhi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. “Muda mwingi nautumia kwenda kwa wananchi na kazi za ardhi zina changamoto kubwa na njia pekee ya kukabiliana nazo ni kutenda haki bila kujali uwezo, kabila ama dini ya mtu,” alisema Hapi.
3
Mafunzo hayo yatakuwa yakitolewa kwa wastani wa saa 56 ya mafunzo kwa maofisa wapya wa matawi mbalimbali ya benki, pamoja na saa 160 kwa mafunzo yatakayokuwa yakiendelea ya darasani kwa maofisa wote wa matawi ya benki hiyo, kila mwaka.Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo uliofanyika katika kituo cha mafunzo ya Benki ya Exim cha ‘Exim Academy’ jijini Dar es Salaam jana, Meneja Mwandamizi wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya Exim, Priti Punatar alisema mafunzo hayo yanalenga katika kuboresha shughuli za matawi katika mazingira yaliyo salama.Alisema pia mafunzo hayo yanalenga kupima ujuzi wa utatuaji wa matatizo mbalimbali bila kuwepo kwa viashiria vya majanga ambayo taasisi za kifedha hukumbana nayo katika masuala ya kibenki.“Wafanyakazi wetu watapewa mafunzo juu ya majukumu mbalimbali katika tawi ili kuwajengea uelewa zaidi juu ya shughuli za kibenki na kuboresha za ujuzi wao katika biashara za masuala ya kibenki. Tunatarajia kuwa njia hii mpya itasaidia kuongeza ufanisi wetu katika shughuli zetu,” alisema Mkuu wa kitengo cha uendeshaji katika benki, Eugene Masawe.Masawe alibainisha kuwa mafunzo hayo yatawawezesha wafanyakazi kujifunza kwa vitendo, mbinu za kuthibitika zitumikazo katika sekta kwa kutumia vifaa vya kipekee, ikiwa pia inalenga katika kuboresha na kurahisisha taratibu za kibenki katika benki.“Tumeanzisha mafunzo haya tukiwa na lengo si tu kuongeza jitihada za kufikia matakwa ya mteja, bali pia kutoa msaada bora wa huduma kwa wateja wetu wote na kuongeza ufanisi na kupunguza makosa yanayojitokeza ya kibenki katika shughuli zetu za kila siku,” alisema Masawe.Alisema mafunzo hayo yataiwezesha benki yake kufikia malengo ya kuendeleza wafanyakazi wa benki hiyo kwa kuwa na ujuzi wa uhakika katika masuala ya kibenki na utoaji wa huduma.
5
ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma, Beatus Kinyaiya amewaasa vijana kutumia elimu yao katika kusaidia taifa na kudumisha amani ya nchi. Aidha, amezitaka familia kudumisha amani, jambo ambalo litasaidia kuwepo kwa amani ya nchi.Askofu Mkuu Kinyaiya aliyasema hayo wakati wa mkesha wa kuzaliwa Yesu iliyofanyika usiku wa kuamkia jana katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Paulo wa Msalaba mkoani Dodoma.Alisema baadhi ya vijana waliopelekwa shule kujifunza wamekuwa chanzo cha uvunjifu wa amani katika jamii kwa kushiriki vitendo vya kihalifu, ikiwa ni pamoja na kuiba kwa kutumia mitandao. “Vijana tumewapeleka shule, lakini mnatumia elimu hiyo kutuvuruga na kutuondolea amani katika jamii. Umepelekwa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kujifunza utaalamu wa kompyuta, mnatumia elimu hiyo kuwaibia watu fedha zao kwenye mitandao, hili ni jambo lisilofaa,” alisema.Alisema sheria za nchi zimewekwa ili jamii iweze kupata amani, lakini bado baadhi ya vijana waendesha bodaboda wamekuwa chanzo cha kuondoa amani kwa jamii kwa kutofuta sheria za barabara. Askofu Mkuu Kinyaiya alisema kuna baadhi ya wanafasalfa waliamini kuwa vita inafaa, na kuwa mawazo kama hayo bado yapo miongoni mwa Watanzania na kusema kuwa hayo ni mawazo ya shetani.“Ukisikia mtu anapenda vita, anapenda ubabe , fujo na watu wakamtetea, inashangaza kidogo; lakini ukichunguza dunia hii hali ya kupenda vita bado ipo, na hili lilianza kuonekana kwa watoto wa kwanza wa Adam na Eva, na hatimaye vita ya mwanadamu na mwanadamu, taifa na taifa. “Mungu alijua uovu na shetani ndio mchochezi na watu wanakubali mawazo yake, ndipo alipoamua kumleta mwanawe Yesu Kristo ili aikomboe dunia, aisaidie kuchana na hali hiyo.” Alisema Yesu alipozaliwa takribani zaidi ya miaka 2000 iliyopita alileta ufalme wa amani na hata alipoanza kuhubiri alihubiri amani na alipofufuka alisisitiza amani kwa wanafunzi wake.“Je, hali imebadilika kiasi gani? Yale mawazo ya wanafasalafa ya kuona vita inafaa bado yanatawala duniani. Familia ngapi zina matatizo kama ya Kaini na Abel, familia moja watu hawapatani.” Askofu Mkuu Kinyaia aliwataka Watanzania kutumia mwaka 2019 kuwa wa mageuzi na kulinda amani katika ngazi ya familia na taifa kwa jumla. “Familia ikipata amani na wote tukimjua Mungu na tukiishi vizuri na taifa litakuwa na amani, kwani wanachoangia kuvuruga amani ni sisi sisi.” Pia alihimza suala la utunzaji wa mazingira na kukemea utupaji wa taka ovyo na kusisitiza kuibadili Dodoma kuwa ya kijani kwa kupanda miti na kwa kufanya hivyo watakuwa wakimsaidia Mungu katika uumbaji na kudumisha amani.
3
Na JOSEPH SHALUWA MKONGWE kwenye muziki wa Hip Hop Bongo, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ ameibuka na kusema kuwa, wasanii  mahasimu wakubwa, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Ali Kiba ndiyo wanauoa muziki wa Bongo Fleva. Profesa Jay ambaye ni Mbunge wa Mikumi, akiwa ameachia ngoma yake mpya ya Kibabe hivi karibuni  amefanya mahojiano na Polisi wa Swaggaz na kuzungumza mengi kuhusiana  na muziki wa Bongo na sanaa kwa jumla. Fuatilia sehemu ya mahojiano hayo; SWAGGAZ: Umeachia ngoma mpya Kibabe, nini kimo ndani ya ngoma hiyo? Kwanini umeiita Kibabe? PROFESA JAY: Nimeuita Kibabe kwa sababu mimi ni msanii mkongwe na nimefanya mengi kwenye huu muziki… na kama nilivyosema humo ndani (ya wimbo), nimechonga barabara ambayo mafanikio hayo (ya muziki) wasanii wengi sasa hivi wanayapata. Mimi ni msanii wa muziki wa juu yaani heavy weight Mc, nimeona kuna baadhi ya mapungufu yapo kwenye game yetu, yakiwemo uandishi, kiki ambazo hazina kichwa wala miguu na vitu vingi vilivyofanya sanaa yetu idorore au ipunguze ule uhalisia wake ambao tulikuwa tunautegemea kila siku. Ndiyo maana nikasema niuite wimbo wa Kibabe, kwa sababu mimi ni msanii mbabe na kama unavyojua hii ni Hip Hop… Hip Hop imejaa majigambo… unajisikia nini moyoni mwako na kupeleka kwa hadhira ambayo ni jamii. Muziki wa sasa hivi ni tofauti sana na zamani sababu mwanzo platforms zilikuwa chache, radio stations zilikuwa chache lakini pia TV zilikuwa chache, studio zilikuwa chache na hata sapoti haikuwa kama ya sasa, lakini sasa hivi kila mtu anasapoti muziki wetu, kuanzia viongozi mpaka mashabiki wa chini, wote wanajitahidi kuwa wazalendo na kusapoti muziki wetu. SWAGGAZ: Unaonaje sanaa yetu na hasa muziki ambao wewe ni msanii wake. Vipi, kuna hatua tunapiga kwenye muziki au unaona tupo palepale? PROFESA JAY: Muziki unakua, lakini wasanii hawapo serious kwenye utendaji wao wa kazi. Unaweza kuona wasanii wakubwa kama Diamond na Kiba ambao wana platform kubwa, lakini hawaongei, mashabiki wao hawasaidiani, hawashirikiani, inachangia sana kuufanya muziki wetu udorore. Naamini kwa nguvu kubwa waliyonayo Kiba na Diamond, wangekuwa pamoja, mashabiki wao nao wangeungana, kama taifa tungeweza kwenda mbele kwa haraka zaidi. Wenzetu Nigeria wameshirikiana sana, watu walikuwa walidhani kuna bifu kati ya WizKid na Davido au D Banj na P Square, lakini baadaye unawakuta pamoja wanakunywa kahawa. Naamini siku moja Diamond na Kiba watamaliza bifu zao na kutengeneza taifa lililo bora na wao kama kioo, kama wasanii ambao tunawaangalia sana, wanaweza kufanya kitu kizuri zaidi. Ushindani ubaki wa kimuziki na siyo wa kishabiki na chuki. SWAGGAZ: Tangu umekuwa mbunge kuna mchango gani mkubwa ulioleta katika sanaa kwa ujumla? PROFESA JAY: Nimefanya mambo mengi ya kuwasaidia wasanii lakini zaidi ni kupaza sauti ya wasanii ndani ya Bunge kutetea haki yetu. Changamoto za wasanii sasa zinajulikana na namna gani ya kubana ili jasho lao liwafikie moja kwa moja. SWAGGAZ: Nje ya bunge, hakuna kitu cha moja kwa moja ulichofanya kwa wasanii? PROFESA JAY: Kama nilivyosema, kazi kubwa nimeifanya kwa kushirikiana na wenzangu, lakini pia studio yangu ya Mwanalizombe nimeihamishia Mikumi na sasa matengenezo yanaendelea ikiwa kwenye hatua za mwisho kabisa. Hii studio itawasaidia wasanii wa Mikumi na hasa wa vijijini kurekodi kazi zao katika quality ya juu. Naamini itakuwa msaada mkubwa sana kwa wasanii wa Morogoro kwa ujumla na wasanii wengine walio katika mikoa ya  karibu kama Dodoma na Iringa na kufanya kazi zao katika viwango bora. SWAGGAZ: Mwelekeo wa muziki wa Tanzania unauonaje kwa sasa hasa katika ushindani wa kimataifa? PROFESA JAY: Mwelekezo ni mzuri, na naamini Kiswahili kinazidi kupasua anga na sisi tunaeleweka. Unaweza kuona sasa hivi wasanii zaidi ya kumi, nyimbo zao zinapigwa kwenye stations kubwa za kimataifa kama Trace, MTV, Channel O nk. Hata Blogs za kimataifa zinaripoti habari zetu, naamini tukiwa wengi, tutazidi kuwa na mafanikio makubwa zaidi. Nayaona mafanikio makubwa mbele yetu. Tukiwa wasanii wengi na channels zikafunguka zaidi, naamini tutazidi kufanya vema kwenye tuzo za kimataifa kama nchi nyingine. Mfano Nigeria unakuta kwenye tuzo nyingi wao wanakuwa 25, Mtanzania mmoja au wawili ndiyo maana wanatushinda, naamini wasanii tukiongezeka tutasaidia zaidi kupasua kimataifa. SWAGGAZ: Unatengaje muda wa muziki na kuwatumikia wananchi bila kuathiri upande wowote? PROFESA JAY: Nasema kila siku, mimi ni mtu wa kutumikia Jimbo la Mikumi kwa asilimia zote. Hii talent nipo nayo, na ninayo kila siku. Nalala nayo, naamka nayo, naoga nayo, nakunywa nayo chai, natembea nayo. Kwahiyo hainizuii hata kidogo kutimiza majukumu yangu jimboni. Muziki ni kipaji, kipo ndani, ninacho siku zote. SWAGGAZ: Vipi kuhusu ndoa yako, baada ya kumvisha mpenzi wako wa muda mrefu pete ya uchumba? PROFESA JAY: Ni kweli Desemba 31, mwaka jana nilimvalisha pete mchumba wangu wa muda mrefu, mama Lissa, anaitwa Grace ambaye nimezaa naye mtoto mmoja Lissa mwenye miaka 11 na Mungu akipenda mwezi wa saba mwaka huu, nitafunga naye ndoa. Naombeni sana baraka zenu, naombeni mniombee ili niweze kulikamilisha jambo hili mbele za Mungu.
1
MWANDISHI WETU- DAR ES SALAAM WAZIRI wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), George Simbachawene amelitaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kutumia ofisi zake za kanda kudhibiti usafirishwaji wa chuma chakavu maeneo yote ye mipaka. Akizungumza mwishoni mwa wiki mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku moja ya kutembelea Bandari ya Dar es Salaam kujionea namna zoezi la usafirishaji wa chuma chakavu inavyoendeshwa, Waziri Simbachawene hakuridhishwa na utaratibu unaotumika sasa kusafirisha chuma chakavu kwani unachangia upotevu wa mapato ya serikali. “Biashara hii inafaida kubwa kwa wafanyabiashara na utaratibu unaotumika sasa kusafirisha chuma chakavu hauisaidii serikali kupata mapato kupitia kodi kwa kuwa hakuna utaratibu wa kutoa risiti,” alisema Waziri Simbachawene. Waziri alisema kuwa katika kipindi hiki ambapo azma ya serikali ni kujenga uchumi wa kati na viwanda ifikapo 2025, chuma chakavu ni moja ya malighafi muhimu zaidi kwa viwanda vya hapa nchini. “Chuma chakavu ambavyo inaruhusiwa kusafirishwa nje ya nchini ‘cast iron’ lakini vyuma vingine vyote lazima vibaki hapa nchini kwani hata viwanda vya ndani vimekuwa na uhitaji mkubwa wa chuma hivyo,” alisema na kuongeza kuwa NEMC lazima wajipange kudhibiti usafirishaji wa chuma chakavu. Simbachawene mbali na kuiagiza NEMC kutumia ofisi zake za kanda, aliwataka wakuu wa mikoa na wilaya kusaidia kudhibiti usafirishaji wa chuma chakavu katika maeneo yao, na hasa mipakani ili kuzuia upotevu wa mapato ya serikali. Aidha, Waziri ametoa muda kwa mamlaka husika kutoa maelezo ya kina kuhusu makontena 18 ya chuma chakavu yaliyosafirishwa nje ya nchi licha ya kuwepo kwa zuio la kusafirishwa makontena hayo. Kwa upande wake Meneja wa Forodha Bandari ya Dar es Salaam, Njaule Mdendu alisema kuwa ziara ya Waziri imetoa mwanga mpya katika kusimamia usafirishaji wa chuma chakavu na kuahidi kufanyia kazi changamoto zake..
3
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafi ri Ardhini (LATRA) inatarajiwa kuingiza mfumo bora wa udhibiti wa mwendo kwa usafi ri wa mabasi nchini utakaosaidia kudhibiti uchezeaji wa vifaa hivyo unaofanywa na madereva.Akizungumza katika mkutano wa dharura ulioit ishwa na Chama cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) kujadili kanuni za usafirishaji wa abiria jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Udhibiti Huduma za Barabara wa LATRA, Johansen Kahatano alisema kwa sasa wapo katika hatua za mwisho kabla ya kifaa hicho kuanza kutumika. Alisema kutokana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika vifaa mbalimbali vya ufuatiliaji wa mwenendo wa mabasi kuchezewa, waliona vyema kuja na kifaa hicho cha kitaifa kwa lengo la kumaliza changamoto hiyo iliyodumu kwa muda mrefu. Alisema hatua ya ujio wa kifaa hicho umetokana na mapendekezo ya baadhi ya wadau mbalimbali walioona kuna haja ya kuwa na kifaa hicho kupunguza kama siyo kumaliza tatizo la ajali zitokanazo na mwendokasi wa mabasi. Alisema kifaa hicho kwa sasa kimepelekwa Shirika la Viwango (TBS) kwa ajili ya uchunguzi wa ubora wake kabla hakijaanza kutumika rasmi wakati wowote kuanzia hivi sasa. Alisema moja ya sifa ya kifaa hicho ni pamoja na kulifanya gari kukata mafuta pale dereva wake atakapokuwa amezidisha mwendo na baadae kuendelea tena ikianza na mwendo wa kawaida.Aidha, aliwataka wamiliki hao kutumia mfumo unatumika hivi sasa wa VTS kwa ufasaha kutokana na umuhimu wake katika kuhakikisha mwendo wa mabasi unakuwa katika viwango vilivyoelekezwa.Awali Katibu Mkuu wa TABOA, Enea Mrutu aliitaka LATRA kufuta baadhi ya vifungu katika kanuni zake ikiwemo ile inayoweza kumfanya mmiliki wa basi kufutiwa leseni kutokana na kosa linaloweza kusababishwa na dereva. Aidha, pendekezo jingine la TABOA ni pamoja na kumtaka dereva kuendesha basi kwa umbali wa kilometa 700 badala ya ile ya kutoendesha baada ya saa nane inayopendekezwa na sheria ya LATRA.
3
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na jamii nzima kwa ujumla wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuendeleza amani na utulivu ili kujenga jamii bora yenye maendeleo.Hayo yamebainishwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alipozungumza na gazeti hili jana kuhusu maadhimisho ya Miaka 42 ya Kuzaliwa kwa CCM yanayoadhimishwa leo nchi nzima. Maadhimisho hayo tofauti na miaka mingine, mwaka huu yanasherehekewa kwa kila mkoa tofauti.Kaulimbiu ya mwaka huu ni; “Kazi ni Kipimo cha Utu, Tuchape Kazi, Linda Uhuru wa Chama” na Polepole amewataka wanajamii kwa ujumla kufanya kazi na kuwa na mikakati ya kujiendeleza kimaisha.Alitumia nafasi hiyo pia kuinadi CCM kuwa imetumia muda wake mwingi kushirikiana na serikali katika kuandaa mazingira bora ya wananchi. Wakati huo huo, uongozi CCM Mkoa wa Dar es Salaam umewataka wanachama wake na wananchi kwa ujumla kushiriki shughuli za kijamii kwenye ngazi za kata, wilaya na mkoa zitakazokuwa zikifanywa na chama hicho.Akizungumza na gazeti hili jana Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa, Kate Kamba alibainisha kuwa mkoa huo umeanza sherehe hizo za chama kwa muda wa wiki moja sasa kwa kufanya usafi na kushiriki kwenye ujenzi wa madarasa kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.
3
IMEELEZWA kuwa hakuna sheria yoyote inayokataza taarifa za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kujadiliwa Bungeni endapo mbunge ataona kuna jambo la kuibua kutoka kwenye taarifa iliyoibuliwa.Akijibu swali la mbunge wa Mgogoni Dk Suleiman Ally Yusuf (CUF), kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William ole Nasha alisema kwamba tume imekuwa ikitimiza wajibu wake na ripoti zake ziwazi. Katika swali lake la msingi, mbunge huyo alikuwa anataka kujua kwa nini ripoti za tume hiyo haziwekwi wazi kwa umma na kama serikali haioni kuwa wakati umefika kujenga utamaduni wa ripoti hizo kujadiliwa bungeni.Naibu waziri huyo alisema kwamba ni kweli kuwa ibara ya 130 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ikisomwa kwa pamona na Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ina ipa tume mamlaka ya kufanya uchunguzi wa uvunjikwaji wa haki za binadamu na baada ya uchunguzi kubaini ripoti zitapelekwa kwa mamlaka husika kwa ajili ya utekelezaji wa maoni ya tume.Aidha sheria inataka tume kuwasilisha taarifa yake ya mwaka katika Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Mawaziri kupitia kwa mawaziri wanaoshughulikia masuala ya haki za binadamu Tanzania bara na visiwani.
3
Wakiingia bungeni mjini Dodoma jana wakati wa kipindi cha Maswali na Majibu, wabunge mashabiki wa timu hiyo, waligonga meza na kwa muda wa dakika moja, shughuli za bunge zilisimama kupisha shamrashamra za mashabiki hao.Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwauliza wabunge kwanini wanagonga meza, kuna nini kimetokea ndipo akabaini kwamba wachezaji wa timu ya Simba, viongozi na benchi la ufundi walikuwa wakingia bungeni ambapo aliwakaribisha akiahidi kuwatambulisha baadaye baada ya kipindi cha maswali na majibu.Wakati akitoa matangazo baada ya kipindi cha maswali na majibu kukamilika, Spika Ndugai aliitambulisha Simba kwamba ipo humo (Bungeni) ikiwa na wachezaji 23, viongozi na benchi na ufundi ambao ni wageni wa Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu (CCM).Wachezaji wa timu hiyo, wakati wakisimama kuwasalimia wabunge ndipo wabunge waligonga meza kwa nguvu zaidi kwa dakika chache na Spika Ndugai akawapongeza kwa kunyakua Kombe hilo. “Nawatakia kila la heri Simba katika kushiriki katika michezo mbalimbali na hatimaye wachukue Kombe la Afrika,” alisema.Kwa ubingwa huo Simba sasa itashiriki michuano ya kimataifa baada ya kukosekana kwa miaka minne. Aidha, Spika Ndugai aliipongeza pia Mbao kwa uchezaji wao na akawaomba waende wakajipande kwa ajili ya msimu ujao ili waendelee kufanya vizuri katika michezo mbalimbali nchini.Lakini pia, Spika Ndugai alimpongeza Mbunge wa Nchemba, Juma Nkamia (CCM) kwa kukumbushia enzi zake za utangazaji kwa kutangaza mchezo huo mbashara kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).Pia alisema, Timu ya Bunge Sports Club inaipongeza Simba Sports Club kwa kushinda mechi ya fainali dhidi ya Mbao FC 2-1 akaitaka Timu ya Mbao wasikate tamaa bali wajipande kwa mashindano ya mwakani.Ndugai aliwapongeza wakazi wa Dodoma na vitongoji vyake kwa kujitokeza kwa wingi kuzishangilia Simba na Mbao katika Uwanja wa Jamhuri wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 17,000 ambao ulijaa pomoni.Pia Spika Ndugai, alisema timu ya Bunge inampa pole mchezaji Jonas Mkude aliyepata ajali juzi wakati akirejea Dar es Salaam kwenda kujiunga na Timu ya Taifa, akataka apone haraka.“Pia timu ya Bunge inasikitishwa na kifo cha mshabiki wa Simba, Shose aliyekufa katika ajali alimokuwa amepanda mchezaji Mkude na naomba roho ya marehemu iwekwe mahali pema peponi,” alisema Spika.
4
Simba inajiandaa kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara na baada ya siku kadhaa za kujifua, timu hiyo itahamishia kambi yake Kisiwani Zanzibar kabla ya kuanza kwa ligi hiyo.Awali, kikosi hicho kilichokuwa kikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Magamba, kilijikuta kikihamishia mazoezi kwenye uwanja wa Chuo cha Irente Rainbow baada ya barabara kuharibika vibaya na kuwa na utelezi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka Lushoto, Simba haitakuwa na mchezo wowote wa kirafiki Lushoto hadi pale timu hiyo itapokwenda Zanzibar kuendelea na kambi yao.Kocha Dylan Kerr anafurahia hali ya hewa ya baridi wakati wachezaji wake wanapiga kelele baada ya wengi wao kuzoea joto kali la jijini Dar es Salaam.“Ukiachana na mambo mengine kama kutopitika kwa barabara wakati huu wa mvua, mimi nimeridhika na hali ya hewa ya hapa,” alikaririwa kocha Kerr.Juzi wachezaji wa timu hiyo waliopo katika kikosi cha timu ya taifa Taifa Stars, walitarajia kujiunga na wenzao kwa ajili ya maandalizi zaidi.Wachezaji hao ni Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Said Ndemla na Hassan Isihaka na Jonas Mkude aliyekuwa Afrika Kusini naye alitarajiwa kutua katika timu hiyo huko Lushoto
4
KAMPENI za kuwania nafasi za uongozi katika Shirikisho la Soka Zanzibar (ZFF) zinatarajiwa kuanza leo visiwani Zanzibar, huku wagombea hao wakihimizwa kufanya kampeni za kistaarabu.Uchaguzi wa ZFF unatarajiwa kufanyika Juni 2 mwaka huu, ambapo kampeni hizo zitafanyika kwa muda wa siku sita zitafungwa siku ya Juni Mosi na jumla ya wagombea 15 wamejitokeza kuomba nafasi mbalimbali, ikiwemo urais, umakamu na wajumbe watano wa Kamati ya Utendaji.Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa ZFF, Fadhil Abrahman Mberwa alisema wakati wa kampeni kamati yao haitaruhusu kuona mgombea mmoja anamchafuwa mwenzake.Alisema kuwa kamati yao ipo makini kwa hilo na iwapo ikithibitika haitakaa kimya na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayefanya hivyo.“Tangaza sera zako kistaarabu usimzungumze mwenzio kwa kumtangazia ubaya, tunataka kampeni za kistaarabu kujenga Shirikisho letu,” alisema.Alisema kuwa kamati inamtaka kila mgombea kutangaza sera zake vyovyote apendavyo lakini si kwa kuchafuana kwani ikitokea hivyo kutaleta athari kubwa umalizapo uchaguzi.
4
MAMII MSHANA Na LEONARD MANG’OHA -DAR ES SALAAM HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam, inatarajia kukabidhi jengo la Machinga Complex kwa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) uliendeshe baada ya kushindwa kurejesha mkopo waliochukua wakati wa ujenzi wa jengo hilo. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa baada ya kufahamishwa kuwa deni na mkopo wa ujenzi wa jengo hilo la kibiashara umefikia zaidi ya Sh bilioni 40 kutoka Sh bilioni 12.7 zilizotumika wakati wa ujenzi wake. “Halmashauri iliingia mkataba na NSSF wa mkopo wa Sh bilioni 10 za ujenzi wa jengo hilo, katika hatua za ujenzi mkataba huo ulifanyiwa nyongeza ya Sh bilioni 2.14 na kufanya jumla ya mkopo kuwa Sh bilioni 12.14, hata hivyo makabidhiano ya jengo hilo yalipofanyika mwaka 2010 gharama za ujenzi zilifikia Sh bilioni 12.7,” alisema Mwita. Alisema wamefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hawana uhakika na uhalali wa deni hilo, ambalo lilipaswa kuwa la ghorofa tano kwa upande mmoja na sita kwa upande mwingine ambapo lingeweza kuhudumia jumla ya wafanyabiashara ndogo ndogo 10,000. Mwita alisema jengo hilo limekabidhiwa likiwa na ghorofa nne huku likiwa na uwezo wa kuhudumia watu 4,206 pekee hali iliyosababisha halmashauri hiyo kushindwa kufikiwa malengo ya kulipa deni na kutoa huduma kwa walengwa. Alisema halmashauri haikuhusika na usimamizi wa fedha zilizokopwa na kuifanya kushindwa kuthibitisha gharama zilizotumika. Aliongeza kuwa kwa mujibu wa mkataba NSSF ilitakiwa kutoa fedha kwa halmashauri kwa ajili ya ujenzi jambo ambalo halikufanyika huku fedha ziliongezwa bila kuwapo makubaliano yoyote kati ya pande hizo. “Kwa muda mrefu halmashauri imekuwa ikijaribu kutafuta mwafaka wa ulipaji wa deni hilo bila mafanikio,” alisema Mwita.
3