text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
Na Mwandishi Wetu-ZANZIBAR MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi na walezi wa Tanzania Zanzibar waache tabia ya kuwaoza wasichana wa kike wakiwa na umri wadogo bali wawasomeshe kwa ajili ya manufaa yao ya jamii kwa ujumla. Kauli hiyo aliitoa juzi kwa nyakati tofauti wakati akizindua madrasa ya kisasa iliyojengwa kwenye eneo la kilimani na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa msikiti mkubwa kuliko yote nchini Tanzania unaojengwa katika eneo la Ijitimai kidoti katika Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa michango ya wananchi katika siku yake ya kwanza ya ziara ya Kikazi Kisiwani Unguja. Alisema kama wazazi na walezi watasomesha watoto wa kike elimu watakayopata itasaidia kwa kiasi kikubwa wasichana hao kufanya maamuzi sahihi na yenye tija katika jamii. “Elimu kuwa ni haki ya msingi kwa mtoto wa kike hivyo ni muhimu kwa jamii nzima ya Zanzibar ihakikishe watoto wa kike wote wanapata elimu kwani watakuwa na uwezo wa kuchagua na kuandaa mustakbali wa maisha yao ya baadaye ikilinganishwa na hali ilivyo sasa kwenye baadhi ya maeneo,” alisema Samia. Kuhusu elimu ya dini, Samia  aliwahimiza wazazi na walezi kuwalea watoto katika maadili mema kwa kuzingatia maandiko matakatifu ya Mtume Muhammad (S.A.W). Alisema vijana wengi wanaolelewa kwa kufuata misingi  bora ya dini ni vigumu kurubuniwa na kujiingiza katika matendo yasiyofaa katika jamii.
3
Na Mwandishi Wetu-Dar es Salaam ALIYEKUWA Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Kipenka Mussa amestaafu kazi ya utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria.   Akizungumza na gazeti juzi, Jaji  Mussa alisema kwa mujibu wa Ibara  ya  120(1) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatamka Jaji wa Mahakama ya Rufani kustaafu kazi hiyo akiwa na umri wa miaka 65. ” Disemba 28, ni siku ya kukumbuka kuzaliwa kwangu,pia siku hiyo  nilistaafu kazi rasmi….namshukuru Mungu nimestaafu kazi hii ya utumishi wa umma niliyoitumikia kwa muda mrefu salama”. Mussa kabla ya kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani na Rais Jakaya Kikwete alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu Kanda mbalimbali ikiwemo  Arusha,  Tanga, Bukoba. Jaji Mussa aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya kuchunguza mauaji ya wafanyabiashara wa madini wa Mahenge . Tume hiyo iliundwa na Rais Kikwete ambayo ilipewa jina la “Tume  ya Jaji Kipenka’  ilimhoji aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam ( ACP- Abdallah Zombe na maofisa wengine wa polisi kwa tuhuma za mauaji ya wafanyabiashara hao. Jaji Mussa aliwahi kuwa Katibu wa Bunge, wakili wa Serikali, Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Haki za Binadamu  ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
3
Djuma aliliambia gazeti hili juzi kuwa hajawahi kuona aina hiyo ya upinzani ambayo ameeleza kuwa ni moja kati ya njia ya kulidhoofisha soka la nchi, kwani inaifanya timu kuhisi kama ipo ugenini.Simba na Yanga zilitupwa nje ya michuano iliyokuwa ikishiriki, lakini Yanga iliyokuwa ikishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika imeangukia kwenye Kombe la Shirikisho huku Simba iliyokuwa ikishiriki Kombe la Shirikisho ikiaga.Djuma, raia wa Burundi alisema kuwa jambo hilo baya ndilo limechangia kwa kiasi kikubwa timu za Tanzania, Simba na Yanga kushindwa kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa.Alisema kuwa kama hilo litakomeshwa kwa mashabiki kujitambua, basi ana imani kubwa timu hizo zitakuwa zikipata matokeo mazuri kwenye uwanja wa nyumbani.“Inaifanya timu kuwa na presha kubwa, Simba inapocheza Yanga inakuzomea halafu Yanga nao ikicheza wanaizomea kitu hicho sio kizuri kwani ndio kimefanya timu zisifanye vizuri mechi za nyumbani…“Ukiangalia hautaweza kupata jibu sijui Yanga ni timu ya nchi nyingine na Simba ni ya nchi nyingine, inabidi kwenye ligi ndio wafanye hivyo lakini kwenye mechi za kimataifa kama hawataki kushangilia basi wakae kimya sio kuzomea,” alisema Djuma.
4
.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa, malipo yote ya korosho kwa msimu uliopita yamekamilika, na sasa serikali inamalizia malipo ya Tani Elfu 25 pekee zilizobaki huku kazi ya kuzisomba korosho hizo kutoka katika maghala mkoani Lindi na Mtwara ikiendelea.Hata hivyo Waziri Mkuu amesema kuwa, Bodi ya Mazao Mchanganyiko imepewa jukumu la kumalizia malipo ya wamiliki wa maghala ya kuhifadhi korosho na madeni mengine yaliyotokana na zoezi hilo.Akisoma hotuba ya kuahirisha mkutano wa 16 wa Bunge jijini Dodoma Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa, tayari serikali imekwishanunua Tani 199 kati ya Tani 222.8 za korosho zote zilizovunwa msimu wa mwaka 2018.Aidha katika kusimamia ununuzi wa korosho kwa msimu wa mwaka huu, Serikali imeweka mazingira ya kuwezesha uwekezaji katika ujenzi wa viwanda vya korosho ili viweze kununua korosho kutoka kwa Wakulima na kuziongezea thamani.Hata hivyo Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa, kupitia wizara ya Kilimo, Serikali inaendelea kuratibu soko la zao la korosho ili kasoro zilizojitokeza katika msimu uliopita zisijitokeze tena msimu huu.
5
Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mtani wake Simba katika mechi ya raundi ya pili ya Ligi Kuu bara iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa juzi.Mabao ya Yanga katika mechi hiyo yaliyovuta hisia za mashabiki wengi yalifungwa na Donald Ngoma na Amisi Tambwe katika kila kipindi.Ushindi huo umeirejesha Yanga kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 46 huku Azam na Simba zikifuatia zikiwa na pointi 45 kila moja.Pluijm alisema baada ya mechi hiyo kwamba ushindi huo haumaanishi kuwa tayari wamechukua ubingwa na kwamba kazi ngumu iko mbele yao mpaka kutetea ubingwa wao.“Angalia bado tuna mechi nyingi za kucheza na nyingi ugenini, tunaenda mechi baada ya mechi, tunafurahi kuifunga Simba lakini bado tuna kazi kubwa,” alisema.Alisema kila timu inataka kuonesha uwezo wake dhidi ya Yanga na hilo linafanya kila mechi wanayocheza kuwa kama fainali. Aidha kuhusu ushindi dhidi ya Simba, Pluijm alisema walishinda kwa sababu walifanya maandalizi mazuri ya kuwaandaa wachezaji kisaikolojia na kimchezo.“Tulijiandaa vizuri, tuliwaandaa wachezaji kimashindano na kisaikolojia na hilo limesaidia kwa kiasi kikubwa kwani kila mchezaji alionekana kujiamini na kuonesha juhudi,” alisema.Pluijm alikipongeza kikosi chake kwa kuonesha mchezo mzuri kama alivyokielekeza akisema kuwa amefurahishwa na matokeo.Pia, aliisifu safu yake ya ulinzi kwa kutendea haki mchezo huo na kufanikiwa kuwazuia wapinzani kushindwa kupenya.Safu ya ulinzi iliongozwa na Vicent Bossou, Mbuyu Twite na Pato Ngonyani tofauti na mchezo wa raundi ya kwanza ambapo iliongozwa na wakongwe Kelvin Yondani na Nadir Haroub ‘Canavaro’.Kocha huyo wa Yanga hakusita kuwazungumzia wapinzani wao Simba kuwa walicheza vizuri pia.
4
['Mshambuliaji wa LA Galaxy Zlatan Ibrahimovic amesema yupo tayari kurejea klabu yake ya zamani ya Manchester United mwezi Novemba.', 'Mshambuliaji huyo mkongwe mwenye miaka 37 amepachika magoli 46 katika michezo 49 toka alipohamia kwenye ligi ya Marekani (MLS) mwezi Machi 2018. ', '"Ninaweza kucheza kwa urahisi kabisa katika Ligi ya Primia. Hivyo, kama United watanihitaji, nipo tayari," amesema. ', 'Ibrahimovic aliifungia Man United magoli 28 msimu wa 2016-17 kabla ya kuandamwa na majeraha ya goti. ', 'Mkataba wake wa miaka miwili na klabu ya United ulivunjwa kwa pande zote mbili kuridhia na kumruhusu kwenda Marekani.', 'Hata hivyo, endapo atafanikiwa kurejea United, atalazimika kusubiri mpaka mwezi Januari ambapo dirisha la usajili kwa ligi ya Uingereza litafunguliwa. ', '"Nimefanya kazi yangu Ulaya. Niliifurahia, nina mataji 33 ambayo nimeyashinda kule, na ninaamini nitashinda kitu hapa. ', '"Baada ya hapo tutaona nini kitafuata na safari itaishia wapi."', 'Ibrahimovic amesema kuwa anaendelea kuangalia mechi za Manchester United na kusisitiza kuwa walikosa bahati walipofungwa na Crystal Palace Jumamosi. ', 'Marcus Rashford alikosa penati wakifungwa na Palace, kama ilivyotokea kwa Paul Pogba wakati wa sare na Wolves siku tano kabla. ', '"Nimeangalia mchezo wa mwisho na naamini hawakuwa na bahati tu," amesema.', '"Kama wakipata penati unakuwa mchezo wa tofauti kabisa, lakini mchezo nchini England hukamilika pale tu kipyenga cha mwisho kinapolia. ', '"Kitu chochote kinaweza kutokea, hususani katika dakika za mwisho wakati joto hupanda kweli kweli."', 'Ibrahimovic pia amebainisha kuwa yungali anawasiliana na Pogba ambaye amekuwa akihusishwa na harakati za kutaka kuihama klabu hiyo. ', '"Naongea nae. Namshauri sana - lakini iwezi kuwambia nyinyi! (waandishi)" alimalizia. ']
4
LONDON, ENGLAND MSHAMBULIAJI wa klabu ya Chelsea, Tammy Abraham, ameweka wazi kuwa, hadi sasa hajafanya maamuzi juu ya kulitumikia taifa gani kwenye michuano mikubwa kati ya England na Nigeria ambapo kila taifa linamuhitaji. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, amekuwa na mchango mkubwa ndani ya klabu ya Chelsea msimu huu ikiwa mchezo wa juzi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Lille akifunga bao moja katika ushindi wa mabao 2-1. Mshambuliaji huyo alizaliwa Camberwell jijini London, lakini ana asili ya nchini Nigeria. Hata hivyo tangu akiwa na umri wa miaka 18 amekuwa akiitumikia timu ya taifa England ya vijana na sasa ni wakati wa kufanya maamuzi ya kuchagua alitumikie taifa gani. Kocha wa timu ya taifa ya England, Gareth Southgate, yupo kwenye mipango ya kumuita mchezaji huyo katika kikosi chake mwezi huu kwa ajili ya kujiandaa na michezo ya kufuzu Euro 2020 dhidi ya Jamhuri ya Czech na Bulgaria, lakini Abraham amesisitiza kuwa hadi sasa hajafanya maamuzi ya nchi ya kuitumikia. “Ni jambo la furaha sana kuona nchi zote zinakuhitaji, ukweli ni kwamba ninazipenda nchi zote, lakini kwa sasa siwezi kulizungumzia hilo, ila kikubwa ambacho ninakiangalia ni jinsi gani ninaweza kuisaidia timu yangu ya Chelsea, ila muda utafikia na kila kitu kitakuwa wazi,” alisema mchezaji huyo. Mchezaji huyo ndani ya klabu ya Chelsea kwa sasa anaanza kufananishwa na nyota wa zamani wa timu hiyo Diddier Drogba kutokana na uwezo wake, hivyo wanaamini atakuwa kuwa na msaada mkubwa kwa kipindi kijacho kutokana na umri wake kuwa mdogo. Timu ya taifa England itashuka dimbani Oktoba 11 dhidi ya Jamhuri ya Czech kabla ya siku tatu mbele kukutana na Bulgaria.
4
BENKI ya Standard Chartered Group imekubali kuipatia Tanzania mkopo nafuu wa Dola za Marekani bilioni 1.46 sawa na zaidi ya Sh trilioni 3.3 kwa ajili ya kujenga kipande cha Reli ya Kiwango cha Kimataifa (SGR) kuanzia Morogoro hadi Makutupora, mkoani Dodoma.Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, ameyasema hayo alipokutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bill Winters, jijini Dar es Salaam."Tunajenga reli hiyo ya kisasa kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Makutupora ambazo ni awamu mbili, pia tutajenga reli hiyo kuelekea Isaka mpaka Mwanza na baadaye Rusumo ambapo wenzetu wa Rwanda, tutasaidiana, wao watajenga reli hiyo kutoka Rusumo hadi Kigali,"amesema.Dk. Mpango amemweleza kiongozi huyo wa Standard Chartered Group anayeongoza benki hiyo kwenye nchi zaidi ya 60 duniani, kuhusu vipaumbele vikubwa vya nchi ikiwemo kuboresha Kampuni ya Ndege Tanzania(ATCL) na ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Mto Rufiji.Amesema Tanzania ni ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii ikitanguliwa na Brazil, lakini inapokea watalii wasiozidi milioni mbili kwa mwaka jambo ambalo linahitaji kufanyiwa kazi kwa haraka ili sekta hiyo ichangie uchumi wa nchi kwa kiasi kikubwa kupitia fedha za kigeni.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered Group, Bill Winters, ameipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa kiuchumi na kwamba benki yake itatoa mkopo huo na kuahidi kuwa balozi wa kuelezea mafanikio makubwa ya kiuchumi ya Tanzania kwa wadau wengine.Ameahidi kuzishawishi taasisi nyingine za fedha ulimwenguni kuangalia uwezekano wa kuunga mkono jitihada hizo ambazo mwisho wake wanufaika wakubwa watakuwa ni wananchi wote wa Tanzania kwa ujumla.
3
NA KULWA MZEE-DAR ES SALAAM SUALA la mfanyabiashara Yusuf Manji kuwa chini ya ulinzi kwa siku 28 katika Hospitali ya Agha Khan limechukua sura mpya baada ya Jamhuri kukana kwa kiapo kwamba haimshikilii mfanyabiashara huyo. Hayo yalidaiwa jana katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mbele ya Jaji Ama–Isario Munisi  wakati maombi ya Manji ya kutaka aachiwe kizuizini kwa sababu anashikiliwa isivyo halali, yalipotaka kuanza kusikilizwa. Mahakama Kuu ilipokea maombi kutoka kwa mawakili wa Manji, Hudson Ndusyepo, Alex Mgongolwa na Jeremiah Ntobesya  wakidai mteja wao anashikiliwa isivyo halali, hivyo wanaiomba mahakama imwachie huru. Lakini Wakili wa Serikali Mkuu, Osward Tibabyekomya,  aliwasilisha majibu ya kiapo kinzani kuhusiana na maombi hayo. Alidai aliwasilisha mahakamani majibu ya viapo viwili kinzani,   kimoja kikiwa kimeapwa na Mpelelezi kutoka Idara ya Uhamiaji, Anord Munuo na   cha pili kutoka ofisi ya Mwananasheria Mkuu wa Serikali, kilichoapwa na Salum Ndalama. Wakili  alidai katika viapo vyote viwili, waapaji wanasema   Manji hashikiliwi na Polisi wala Uhamiaji. Akijibu, Wakili Mgongolwa alidai Manji anashikiliwa na Uhamiaji na analindwa na polisi kwa siku 28 sasa. Alisema  walipofika kwa mara ya kwanza mahakamani walinzi hao walitumia gari lake kumfikisha mteja wake mahakamani. “Mheshimiwa Jaji, hata leo Manji kaletwa chini ya ulinzi, askari wamemfikisha mahakamani wenyewe wakakaa nje. “Mara ya kwanza walitumia gari langu…hata leo walitaka kutumia gari langu lakini wakaamua kumleta na gari lao. “Mheshimiwa Jaji, Manji analindwa na polisi sita, tunaomba tupewe muda wa kujibu majibu ya kiapo kinzani na iwekwe kwenye kumbukumbu za mahakama kwamba hashikiliwi kama wanavyodai Jamhuri. “Sisi hatuwezi kuwa wendawazimu tulete maombi mahakamani kuomba aachiwe kizuizini wakati hajashikiliwa,”alidai Mgongolwa. Jaji Munisi alisema majibu ya kiapo kinzani yote mawili yanaeleza kwamba Yusuf Manji hajashikiliwa. “Nashangaa, najiuliza maswali kwa nini Jamhuri wanasema hawajamshikilia?  Waleta maombi wanasema anashikiliwa…!
3
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ameliagiza Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kushirikiana na Jeshi la Polisi kumkamata na kumweka ndani Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Tumaini Godfrey a.k.a. Dudu Baya kwa kukejeli na kumdhihaki hayati, Ruge Mutahaba.Msanii Dudubaya jana alijirekodi katika clip na kuisambaza mitandaoni akionesha kuulizia wasanii waliokufa siku zilizopita kama Ruge amefika huko, kwani aliwazurumu watu na kawatesa…. Anaelekea kwenye mlango wengi au kapita pembeni aa kumbe wa kushoto…. Akifungua Mkutano wa Kazi wa 11 wa Maofisa Utamaduni nchini uliofanyika jijini hapa, Waziri Mwakyembe alisema, kitendo cha msanii huyo cha kukejeli kifo cha Mutahaba si cha utamaduni wa Watanzania.Dk Mwakyembe alisema huwezi kukejeli kifo cha Ruge, ndio maana hata Rais John Magufuli alikuwa mtu wa kwanza kutwiti akionesha masikitiko makubwa kutokana na kifo cha Mtendaji Mkuu wa Clouds Media, Ruge.“Nimesikitika sana, msanii wa siku nyingi unamkejeli mwenzako, hujui ni Watanzania wangapi wameumia kuhusu kifo hicho... Hujui ukipita barabarani utakuwa salama kiasi gani… Tukakuhifadhi mahali ili akili yako ikae vizuri…ili kumlinda yeye sheria inaturuhusu kabisa. “Mimi naagiza Msaniii huyo achukuliwe hatua kali za kinidhamu … Nami nategemea ndani ya saa mbili awe amechukuliwa hatua.Huu si utanzania tukianza kuruhusu upuuzi huo, haiwezekani… “Nimeumia sana, mwanangu amefanya kazi kubwa ametanguia mbele ya haki, sisi tunakuwa wapuuzi sisi… Hatuwezi kukubali hilo… Hiki ni kipindi cha kuliwazana si kipindi cha kumrushia marehemu vijembe na kuweka madai mbalimbali… Msanii huyo nachokifanya si kizuri.“Kuna watu wameumia sana na mimi mwenyewe nimeumia sana… Huu si utamaduni wa Kitanzania… kufanya hivyo mtu unahatarisha kuondoa amani katika jamii…” Dk Mwakyembe alisema kipindi hiki ambacho watu mbalimbali nchini wanaomboleza kifo cha Ruge kilichotokea Afrika Kusini, msanii huyo amerusha vijembe, kitendo ambacho si kizuri kumrushia vijembe maiti, kitendo hicho kinaweza kuondoa amani kwa jamii.Alisema kutokana na kitendo cha msanii huo ni vema Basata wapeleke malalamiko hayo polisi na ndani ya saa mbili msanii huyo awekwe mahabusu ili kulinda usalama wake. Dk Mwakyembe alisema Ruge ametoa mchango mkubwa katika kuelimisha umma, mchango ambao msanii Dudu Baya anaweza asiutoe hata katika kipindi cha miaka 100 ijayo. Taarifa zingine zilizopatikana baadae jana zinasema kuwa, Dudubaya alijisalimisha mwenyewe katika Kituo cha Polisi Oysterbay, ambako amehifadhiwa.
4
Na RAPHAEL OKELLO MKUU wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili, ameliagiza jeshi la polisi kuwakamata na kuwafikisha mahakamani wazazi na walezi ambao watoto wao wanajihusisha na ajira   migodini. Alisema lengo ni  kukomesha uvunjaji wa haki za watoto. Akizungumza na wachimbaji wa Kijiji cha Kamkenga jana, Bupilipili alisema agizo hilo linahusisha   wamiliki wa migodi ambao wamekuwa na tabia ya kuwaajiri watoto na kuwatumikisha biashara au kufanya kazi mbalimbali za ndani badala ya kuwapeleka shule. “OCD nakuagiza kuanza sasa mtoto yeyote atakayepatikana mgodini akifanya kazi mkamate ili amtaje  mzazi wake naye akamatwe. “Lakini aliyempa ajira hiyo naye hakikisheni anakamatwa kwa sababu   wanawachochea watoto kuacha shule  na kujiingiza katika biashara hizi,” alisema Bupilipili. Alisema mtoto anapaswa kusoma shule na siyo ajira, hivyo haiwezekani wazazi kuwatumikisha watoto ili wapate riziki kwa kisingizio cha hali ngumu ya maisha. DC alisema watoto  hata wakiwa kwenye ajira hawana uwezo kujadiliana  na mwajiri kupata malipo stahiki lakini pia ni kinyume na sheria.   Bupilipili  pia alitangaza kufunguliwa  mgodi  wa Kamkenga ambao ulifungwa kwa takribani wiki moja kupisha  ukaguzi wa usalama  wa mgodi. Alisema  shughuli  za uchimbaji ziliruhusiwa katika  maduara 22 yaliyothibitishwa  kuwa  salama na mengine 44 yakiagizwa kufanya marekebisho kadhaa  kabla ya serikali kuruhusu shughuli hizo kuendelea.
3
NA CHRISTINA GAULUHANGA -DAR ES SALAAM WAAJIRI nchini wametakiwa kuhakikisha wanalipa malimbikizo ya michango ya wafanyakazi wao kabla ya Juni 30, mwaka huu ili kuepuka kufikishwa mahakamani. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa  Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bathow Mmuni, alisema waajiri watakaolipa malimbikizo yao ya michango ndani ya Mei na Juni mwaka huu watasamehewa tozo za malimbikizo kwa asilimia 100. “Waajiri watakaolipa tozo (penati) za malimbikizo yao wanazodaiwa na shirika kwa asilimia  50 ndani ya kipindi hiki watasamehewa asilimia 50 ya tozo iliyobaki,” alisema Mmuni. Alisema msamaha huo utaanza Mei 2, mwaka huu na kuishia Juni 30, mwaka huu. Mmuni alisema fedha hizo zikipatikana zitasaidia kuendeleza miradi na kujenga viwanda. Pia alisema wanatarajia kufunga mwaka wa fedha Juni mwaka huu hivyo ni vyema kila mwajiri akaleta malimbikizo yake. Mmuni alisema wamepanga kukusanya kiasi cha Sh bilioni 23 kutoka kwa waaajiri  ambazo ni malimbikizo ya michango yao. Aliongeza kuwa katika kuhakikisha oparesheni hiyo inafanikiwa wakaguzi watapita katika ofisi mbalimbali kuzungumza na waajiri ili malipo yafanyike kwa wakati. Mwisho Balozi Seif aongoza dua kuombea amani Z’bar Na Othman Khamks Ame, OMPR MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, alisema mkusanyiko wa waumini wa dini ya kiislamu katika mfumo wa kushikamana bila ya kufarakana daima huzaa baraka zinazootesha neema na heri kwa umma na mbele ya Mwenyezi Mungu. Kauli hiyo aliitoa juzi wakati wa dua maalumu ya kuliombea taifa amani na utulivu pamoja na kujiandaa kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuingia wiki chache zijazo. Dua hiyo ilifanyika katika Msikiti wa Ijumaa Malindi mjini Unguja na kuhudhuriwa na mamia ya waumini wa dini ya Kiislamu na baadhi ya wiongozi wa Serikali. Alisema waumini na wananchi wote wanapaswa kuzingatia  umuhimu wa suala la amani iliyopo nchini kwani kwa kufanya hivyo kutatoa fursa kwa waumini hao kutekeleza kwa utulivu ibada zao sambamba na kuendelea na harakati zao za maisha za kila siku. Balozi Seif alitoa wito kwa wafanyabiashara wote kuacha tabia ya kupandisha bei za bidhaa muhimu zinazotumiwa kwa wingi na waumini wa dini ya kiislamu katika kipindi hicho cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Alisema tabia hiyo mbaya ni dhambi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haitakuwa na huruma katika kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara  watakaopandisha bei za bidhaa bila sababu za msingi. Mapema Mufti Mkuu wa Tanzania Bara,  Sheikh Abubakar  Zubeir Ali,  alisema dua ni fursa kubwa inayompa  mwanadamu kumuomba Mungu amwelekeze katika njia ya amani.
3
KWA mara ya mwisho Tanzania ilishiriki fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani (Chan) mwaka 2009, ikiwa ni miaka 10 sasa tangu wakati huo.Fainali hizo za Chan zilikuwa za kwanza kufanyika tangu kuanzishwa na Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) zikiwa na lengo la kuwawezesha wachezaji wa bara hili wanaocheza soka nyumbani, ili nao kupata nafasi ya kuonesha vipaji vyao.Caf ilibaini kuwa mataifa yaliyokuwa yakishiriki michuano ya kawaida ya Mataifa ya Afrika (Afcon) mengi vikosi vyao vilikuwa vikiundwa na wachezaji wengi wanaocheza soka nje ya nchi zao, hivyo wale wa nyumbani walikuwa hawapati kabisa nafasi ya kuonekana.MASHINDANO YA KWANZAMashindano ya kwanza ya Chan yalifanyika mwaka 2009 na Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi nane zilizofuzu kushiriki fainali hizo ikiwemo mwenyeji Ivory Coast. Mbali na Tanzania na Ivory Coast, nchi zingine zilizoshiriki fainali hizo ni pamoja na Libya, Senegal, Ghana, DR Congo, Zambia na Zimbabwe.Tanzania ilipangwa katika Kundi A pamoja na Zambia, Senegal pamoja na wenyeji Ivory Coast, ambapo ilishinda mechi moja dhidi ya Ivory Coast (1-0), ikatoka sare ya 1-1 na Zambia na kufungwa 1-0 na Senegal na kumaliza ya tatu katika kundi lake ikiwa na pointi nne.Zambia ndio ilikuwa ya kwanza katika kundi A kwa kumaliza na pointi tano sawa na Senegal, hivyo Tanzania ilikosa pointi moja tu nayo kufikisha pointi tano kama Zambia na Senegal ambazo zilicheza nusu fainali.KIKOSI CHA STARS 2009Kikosi cha Taifa Stars kama mataifa mengine kilikuwa na wachezaji 23, ambao walishiriki fainali hizo, ambao ni:- Deogratias Munishi , Salum Swedi, Haruna Moshi, Athuman Idd, Kelvin Yondan, Henry Joseph Shindika, Kigi Makasi, Mrisho Ngasa, Geofrey Bonny, Jerson Tegete, Musa Mgosi, Nurdin Bakari na Nadir Haroub. Wachezaji wengine ni pamoja na Shadrack Nsajigwa, Abdi Kassam, Nizar Khalfan, Amir Maftah, Shaban Dihile, Shaban Nditi, Farouk Ramadhan, Juma Jabu, Erasto Nyoni na Mwinyi Kazimoto.Kikosi hicho kilikuwa chini ya kocha Mbrazil Marcio Maximo. Tanzania tangu mwaka 2009 tangu wakati huo haijawahi tena kushiriki fainali hizo za Chan, na sasa harakati zinaanza kesho Jumapili kwa kucheza na Kenya, Harambee Stars katika mchezo wa kufuzu.MBIO ZA CHAN 2020Fainali za Chan 2020 zitafanyika nchini Cameroon na Tanzania inakutana na Kenya kesho Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kusaka nafasi ya kwenda Cameroon kwa fainali hizo. Ni mpambano wa aina yake kwani endapo Taifa Stars itashinda na kuitoa Kenya, basi itatinga raundi ya mwisho ya kufuzu kwa kucheza dhidi ya Sudan.Taifa Stars iko kambini chini ya kocha wa muda, Ndiliagije, ambaye amechukua nafasi ya Mnigeria Emmanuel Amonike ambaye alitimuliwa kazi baada ya Taifa Stars kuvurunda katika Michuano ya Mataifa ya Afrika, Afcon 2019 nchini Misri. Kambi ya timu hiyo iko Boko jijini Dar es Salaam na kocha amehakikisha kuwa Taifa Stars ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri na kuitoa Kenya na kusonga mbele.DENI KWA KENYATanzania ina deni kubwa kwani kwani katika Afcon 2019 iliyomalizika wiki mbili zilizopita, ilifungwa 3-2 katika hatua ya makundi huko MIsri, hivyo huu ni wakati wa Taifa Stars kulipa kisasi kwa Wakenya. Taifa Stars ya Chana haina tofauti sana na ile ya Afcon kwasababu kikosi chao kilikuwa na wachezaji wengi wanaocheza ligi ya nyumbani, hivyo wachezaji wengi watakuwa ni wale wale.Wachezaji wetu wamezoena, hivyo ni matarajio ya wengi kuwa kocha hatakuwa na kazi ngumu ya kuwaunganisha na hilo litasaidia sana kucheza kitimu na kuleta ushindi. Pia kikosi hicho kina wachezaji wazoefu kama Kipa Juma Kaseja, ambaye licha ya kuwemo katika kikosi kilichoiwezesha Taifa Stars kufuzu kwa Chan 2009, hakuwemo katika fainali za Ivory Coast baada ya kutoelewana na Maxime.NAFASI KWA STARSNa kama Stars itavuka na kufuzu kwa mara ya pili kucheza fainali za Chana 2020, basi hakuna ubishi tutakuwa na nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwani timu yetu itakuwa na wachezaji waliozoeana zaidi ukilinganisha na wenzetu. Na hii ndio maana katika fainali za Chan 2009 tuliifunga timu kama Ivory Coast na kutoka sare na Zambia kwakuwa Tanzania ilikuwa inaundwa na wachezaji wenye uzoefu wa mashindano ya kimataifa, kwani wachezaji wetu ndio hao hao tulikuwa tukiwatumia kwa mashindano mengine ta kimataifa, tofauti na wenzetu.Mataifa mengine yenyewe katika mashindano mengine kama ya kufuzu kwa Kombe la Dunia, yale ya kufuzu kwa Afcon na fainali zake, wamekuwa wakiwatumia wachezaji wao wanaocheza Ulaya, lakini kwa Chana wanawatumia wale wa nyumbani kutokana na kuibanwa na kanuni.MASHABIKI WAISHANGILIEMashabiki ambao ni mchezaji wa 12 wasisite kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuishangilia timu yetu ili iweze kuifunga Harambee Stars kwa mabao mengi na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.Baada ya kushindwa kufanya vizuri Afcon 2019, sasa Taifa Stars ina deni la kulipa kwa mashabiki na taifa kwa ujumla ili kuwafuta machozi wapenzi wa soka nchini. Tunatakiwa kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yetu ili iweze kufanya vizuri na kupata nafasi ya kucheza raundi ya mwisho ya kufuzu dhidi ya Sudan na hiyo tukiifungisha virago, basi tutakuwa tumefuzu kwenda Cameroon. Watanzania tusichoke kwenda kuishangilie Taifa Stars, kwani nguvu na ari tuliyokuwa nayo wakati wa kufuzu kwa Afcon 2019, basi tuwaoneshe wachezaji wetu wa Chan.
3
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeelezea masikitiko yake kutokana na kifo cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, ikisema ameacha pengo kubwa katika tasnia ya habari.Hayo yalisemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mihayo Juma N’hunga wakati akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika duniani kote jana. N’hunga alisema Dk Mengi atakumbukwa kwa mambo mengi mema akiwa miongoni mwa wawekezaji wa mwanzo kuitumia fursa ya kuanzishwa vyombo vya habari nchini.Alisema hatua hiyo kwa kiasi kikubwa imesaidia uwekezaji katika sekta hiyo ikiwemo ajira kwa waandishi wa habari wanaomaliza elimu kwa viwango mbalimbali. “Kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar natoa salamu za masikitiko kufuatia kifo cha mfanyabiashara maarufu na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dk Reginald Mengi ambaye ametumia muda wake mwingi katika kuwekeza kwenye sekta ya habari na ajira,” alisema Naibu Waziri N’hunga.Aliwataka waandishi wa habari na wawekezaji wengine kuiga mfano wa Mengi aliyetumia utajiri wake kwa ajili ya uwekezaji na kutoa ajira kwa watu wengine. “Watu wengine ikiwemo matajiri waige mfano wa Mengi katika kutumia utajiri wake kwa ajili ya kuwanufaisha wengine,” alisema. Aidha, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Hassan Mitawi alisema baraza litamkumbuka Mengi kwa ushirikiano wake mkubwa kwa vyombo vyake vya habari ambavyo vimetoa mchango wa hali ya juu katika uhuru wa vyombo vya habari.Alisema wakati waandishi wa habari wakiadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani wanatakiwa kukumbuka mchango wa Dk Mengi aliyesaidia kwa kiasi kikubwa kuimarisha taaluma ya uandishi wa habari nchini. “Mengi tutamkumbuka kutokana na mchango wake mkubwa katika kuimarisha taaluma ya uandishi wa habari nchini sambamba na uhuru wa taaluma hiyo ikiwemo kutoa ajira kubwa kwa waandishi wa habari,” alisema. Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake (Tamwa) Zanzibar, Dk Mzuri Issa alisema taaluma ya uandishi wa habari imepata pigo kubwa kutokana na kifo cha Dk Mengi.
3
TANZANIA imeendelea kufanya vizuri katika soko la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kutokana na bidhaa zake mbalimbali kufanya vyema huku ikijipanga kutambulisha nyingine mpya.Wakati chai, kahawa, pamba, vigae, saruji na dhahabu ni miongoni mwa bidhaa zinazouzwa katika soko, bidhaa mpya zinazotarajiwa kutambulishwa ni mazao ya kilimo hususani korosho, mifugo, chuma na mazao ya bahari.Kaimu Mkurugenzi wa Viwanda katika Wizara ya Viwanda na Biashara, Abdul Marwa alisema hivi karibuni kwamba thamani ya mauzo ya Tanzania katika soko la SADC mwaka jana ilikuwa dola za Marekani milioni 999.34 ikilinganishwa na dola milioni 877.8 za mwaka juzi.Marwa ambaye alikuwa akitoa mada katika mafunzo kwa waandishi wa habari yaliyofanyika mkoani Morogoro kuwajengea uwezo katika kuripoti habari za SADC, alisema ongezeko hilo la asilimia 12.16, ni zaidi ya mara mbili ya mauzo katika soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Katika soko la Afrika Mashariki, mwaka jana Tanzania iliuza dola za Marekani milioni 448.5 ikilinganishwa na dola za Marekani milioni 312.5 sawa na ongezeko la asilimia 43.6.Alisema nchi imejizatiti kuwekeza zaidi katika bidhaa za kilimo katika soko hilo la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika inayoundwa na nchi wanachama 16. Wakuu wa serikali na nchi hizo wanachama watakutana mwezi ujao Dar es Salaam.Akizungumzia wiki ya viwanda ya SADC itakayoanza Agosti 5 hadi 8 kabla ya mkutano wa 39 wa wakuu wa serikali na nchi, Marwa alisema ni sehemu ya matukio muhimu ambayo Watanzania watapata fursa ya kutangaza bidhaa zao. Alisema wiki hiyo ya maonesho ya viwanda, inatokana na mkakati wa viwanda wa SADC wa mwaka 2015-2063 unaolenga kuongeza kasi ya kuimarisha ushirikiano na ushindani wa kiuchumi kwa nchi wanachama hususani katika viwanda na biashara.Alipofungua maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alisema mwaka 2017/18, Tanzania ilifanya vizuri katika mauzo yake kwenye soko la EAC, SADC na Umoja wa Afrika (AU). Makamu wa rais alisema katika SADC iliuza kwa asilimia 29.8, EAC asilimia 10.63 na AU asilimia 5.6. Alisema nia ya serikali ni kuongeza wigo mpana zaidi wa bidhaa za Tanzania katika nchi wanachama wa jumuiya hizo.
3
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM SIKU moja baada ya kuuawa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma,  Amedeus Malenge, watu wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo wametiwa mbaroni. Watuhumiwa hao walikamatwa usiku wa kuamkia jana, Kinyezi Kanga   Dar es Salaam, baada ya msako mkali uliohusiha askari wa kikosi maalumu kutoka Kanda Maalumu ya Dar es Salaam. Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi kiliambia MTANZANIA jana kuwa watuhumiwa hao walikamatwa baada ya kuhusishwa na tukio hilo la mauji ya kinyama. Malenge ambaye ambaye alihamishiwa wilayani Uvinza akitokea Kibaha mkoani Pwani ambako alikuwa Ofisa Upelelezi wa wilaya, aliuawa   juzi   saa 4.00 usiku.  “Ni kweli wamekamatwa baada ya msako mkali wa polisi,” alisema mtoa taarifa huyo ambaye hakutaja kutajwa jina gazetini kwa kuwa si msemaji wa polisi  na kuongeza: “Marehemu alikuwa anapita na gari yake jirani ya nyumba yake moja ambayo bado haijaisha. Akiwa katika hilo eneo alimuona mtu mmoja ambaye walikuwa wakifahamiana akilalamika kuwa kuna watu walikuwa wanataka kumuua huku akimwita kwa jina ili amsaidie. “Marehemu aliposhuka   aliuliza ‘kulikoni mbona mnataka  kumpiga, kulikoni’. “Ghafla alitokea mtu kwa nyuma akampiga kwa shoka kichwani   akafariki papo hapo”.   MTANZANIA ilipomtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilipolisi wa Ilala, Salum Hamduni   kupata ufafanuzi wa suala hilo, simu yake ilipokewa na msaidizi wake ambaye alisema alikuwa  kwenye majukumu ya kazi. “Mimi si kamanda ila mimi ni msaidizi wake, kamanda yupo kwenye majukumu na kama unamhitaji atakupigia baada ya muda wa dakika 10 kutoka sasa,” alisema msaidizi huyo wa Kamanda Hamduni na kukata simu.
3
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM JOPO la madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) waliomfanyia vipimo vya uchunguzi motto, Shukuru Kisonga (16), leo litatoa ripoti kueleza kile walichokibaini. Mtoto huyo amekuwa akilazimika kula mafuta ya kula lita moja, maziwa lita mbili na robo tatu ya kilo ya sukari ili aishi kama watu wengine na akivikosa vitu hivyo hupata maumivu makali mwilini. Akizungumza na MTANZANIA jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja, Aminiel Aligaesha,  alisema  uchunguzi wa madaktari umekamilika. “Juzi walimchukua damu na kufanya vipimo mbalimbali, ilikuwa watoe taarifa hiyo leo (jana) lakini wameomba waitoe kesho (leo),” alisema. Shukuru na mama yake, Mwanabibi Mtete, walifika Hospitalini   kutoka nyumbani kwao Tunduru mkoani Ruvuma kwa agizo la serikali baada ya taarifa zake kusambaa katika mitandao mbalimbali ya  jamii. Akizungumza na waandishi wa habari, Mwanabibi alisema iwapo Shukuru akikosa vitu hivyo vitatu mwili wake huwa kama gari lililoishiwa mafuta. “Huwa anapata maumivu makali, anakuwa kama anajikata kata, natumia mikono yangu kumsaidia, sasa mimi ni mjane maisha yangu ni duni nilikuwa napata wakati mgumu kumsaidia mwanangu,” alisema. Alisema Shukuru ni mwanafunzi wa kidato cha pili wilayani humo na   hali hiyo inapomtokea wenzake shuleni hulazimika kumbeba na kumrudisha nyumbani.
3
Akizungumza jijini hapa, Mwenyekiti wa Kamati ya Madini ya Vito Tanzania, Gregory Kibusi, alisema: “Wachimbaji wa madini ya vito na usonara, watarajie kupata masoko ya madini yao nje.“Wanunuzi wa bidhaa zetu wapo na wana imani kubwa na madini yetu. Jambo kubwa tulilolihitaji ilikuwa kujua masoko na namna ya kupata taarifa mbalimbali. Tunafurahi kwa hilo, tumefanikiwa.”Akizungumzia namna alivyonufaika na maonesho hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Madini ya H.B, Harry Mushi alisema maonesho hayo yamewasaidia kujua nafasi zao kibiashara.Aliongeza, maonesho hayo yamewasaidia kujua aina za madini zinazotakiwa kuwasilishwa kwenye maonesho ya kimataifa, na umuhimu wa kuzingatia ubora wa madini.“Tumegundua wafanyabiashara wa madini Tanzania tunahitaji kujipanga ili kuliteka soko la kimataifa. Tumejifunza umuhimu wa kukata madini. Madini tunayo na ni bora sana. Wachimbaji wanatakiwa kuyaongezea thamani madini yao. Jambo hili ni muhimu sana, tunahitaji kujipanga,” alisema.Naye mfanyabiashara wa madini na Ofisa Masoko wa kampuni ya Tom Gems, Jeremiah Simeon, ameshukuru Serikali ya Tanzania kutokana na kuwa na uhusiano mzuri na Thailand uliowezesha wafanyabiashara wa Tanzania kushiriki maonesho hayo na kuwafungulia mipaka ya ufahamu kuhusiana na biashara ya madini ya vito na usonara katika ngazi za kimataifa.Akizungumzia ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo, Kamishna Msaidizi wa Madini, Hamis Komba, alisema Serikali ina mengi iliyojifunza kutokana na ushiriki wake katika maonesho hayo ikiwemo matumizi ya teknolojia zinazotumika katika sekta hiyo.Akizungumzia kuhusu uthamini wa madini ya vito na almasi katika maonesho hayo, mthamini wa madini kutoka idara ya uthamini wa madini ya almasi (TANSORT), Edward Rweyemamu alisema idara ya uthamini imeyatumia maonesho hayo kutafiti mwenendo wa bei za madini, jambo ambalo litawasaidia kuifanyia marekebisho kanzidata ya bei ili kuhakikisha wanapata mrahaba stahiki.
5
Ni ushindi wa tatu mfululizo kwa timu hiyo katika ligi hiyo, lakini ukiwa ni ushindi wa pili tangu Simba imuondoe Kocha Mkuu wa timu hiyo, Dylan Kerr raia wa Uingereza na nafasi yake kukaimiwa na Mganda, Jackson Mayanja.Jumamosi Simba ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja huohuo, ikiwa ni mchezo wa kwanza tangu iwe chini ya Mayanja, ingawa ulikuwa wa pili mfululizo kushinda baada ya awali kuifunga Ndanda FC bao 1-0 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara.Kutokana na ushindi huo wa jana, Simba sasa imefikisha pointi 33 katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiendelea kushika nafasi ya tatu nyuma ya Yanga yenye pointi 36 na Azam inayoongoza ikiwa na pointi 39.Azam imechukua usukani wa ligi jana kutoka kwa Yanga, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wake dhidi ya Mgambo Shooting uliofanyika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.Hata hivyo msimamo wa ligi hiyo unaweza ukabadilika leo, wakati Yanga itakaposhuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza na Majimaji ya Songea, ambapo kama itaibuka na ushindi itarejea kileleni kutokana na kuwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.Katika mchezo wa jana, Simba ilibidi isubiri hadi dakika ya 52 kushangilia bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti mfungaji akiwa Hamis Kiiza baada ya Danny Lyanga kukwatuliwa eneo la hatari.Dakika kumi baadaye, Simba walipata bao la pili mfungaji akiwa Lyanga baada ya kuwatoka mabeki wa JKT Ruvu, bao lililoibua shangwe kutoka kwa mashabiki wa timu hiyo. JKT Ruvu inayonolewa na kocha wa zamani wa Simba, Abdallah Kibadeni ilijitahidi kucheza kwa nguvu, lakini umaliziaji haukuwa mzuri kwa washambuliaji wake kushindwa kulenga lango kila walipokaribia eneo la hatari.Simba SC; Vincent Angban, Emery Nimubona, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’/Abdi Banda, Hassan Isihaka, Juuko Murushid, Justice Majabvi, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude, Hamisi Kiiza, Daniel Lyanga/ Raphael Kiongera na Peter Mwalyanzi/Hassan Kessy.JKT Ruvu; Hamisi Seif, Michael Aidan, Paul Mwidivi, Sesil Efrem, Nurdin Mohammed, Naftari Nashon, Hassan Dilunga, Issa Ngao/ Amos Mgisa, Samuel Kamuntu/ Saad Kipanga, Hamisi Thabit/Najim Magulu na Mussa Said.Naye Alexander Sanga anaripoti kuwa Stand United jana iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Toto Africans kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga. Kutokana na ushindi huo, Stand United imepaa kwa nafasi moja kutoka ya tano iliyokuwepo mwanzo na kuishusha Mtibwa Sugar baada ya kufikisha pointi 28.Mtibwa ina pointi nne. Bao la kwanza la Stand United lilifungwa dakika ya 21 na Vitalis Mayanga kutokana na mpira wa adhabu wa Nassor Said na kumshinda kipa Mussa Mohammed.Stand walipata bao la pii dakika ya 38 mfungaji akiwa Selemani Kassim ‘Selembe’ kutokana na pasi ya Selemani Mrisho, wakati bao la Toto lilifungwa dakika ya 80 na Miraji Makka kutokana na mpira wa adhabu uliomshinda kipa Frank Muwonge.Mchezaji wa Toto Africans raia wa Ivory Coast Assouman David alipewa kadi nyekundu na mwamuzi kutoka Kagera, Ahamada Simba kutokana na kumchezea vibaya Japhet Vedastus.Kutoka Tanga, Mwandishi Wetu anaripoti kuwa Azam iliifunga Mgambo Shooting mabao 2-1, hivyo kukalia usukani wa ligi hiyo kwa muda wakati wakisubiri hatima ya mchezo wa Yanga na Majimaji leo.Mabao ya Azam jana yalifungwa na beki wa kulia wa timu hiyo Shomary Kapombe, wakati lile la Mgambo ambayo Jumamosi iliifunga JKT Ruvu mabao 5-1 Uwanja wa Karume, Dar es Salaam lilifungwa na Bolly Shaibu.Katika mechi nyingine zilizochezwa jana, Prisons iliifunga Coastal Union mabao 2-1 Uwanja wa Sokoine Mbeya, huku Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, wenyeji Ndanda waliifunga Mbeya City mabao 4-1.
4
Kaimu Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Ombeni Zavalla alisema jana kuwa, timu hiyo yenye wachezaji 27, wakiwemo 16 wa kiume itaweka kambi Shule ya Filbert Bayi, Kibaha mkoani Pwani. Alisema kambi hiyo ambayo awali ilitakiwa kuanza Aprili Mosi, imechelewa kuanza kutokana na ukata unaoiandama RT.Aliongeza kuwa, kwa sasa bado wanatembeza `bakuli’ kuomba msaada kwani kinahitajika kiasi cha Sh milioni 45 kwa ajili ya kambi na mashindano.Timu hiyo itakuwa chini ya makocha Robert Kaliyae, Mwinga Mwanjala na Epifania Mugaga wakati meneja ni Peter Mwita.Wanariadha wa kike wanaounda timu hiyo ni Rehema John, Jane Maiga, Hynes Nampenja, Dorcas Boniface, Bitrina Michael, Esther Martin, Angelina Tsere, Eunice Mussa, Rose Seif na Aisha Mohammed.Wanaouunda timu ya wanaume ni Benjamin Michael, Oscar Prosper, Adnani Haruna, Imani James, John Sirima, Sabas Daniel, Jackson Makome, Thobias Bura, Simon Francis, Emmanuel Gadie, Francis Dambel, Hafidh Khalfan, Anthony Mwanga, Dennis David na Jimmy Kusumo.
4
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wazalishaji wa vinywaji, vileo na mvinyo mkoani hapa kufunga mfumo wa stempu kodi za kielektroniki ifi kapo mwishoni wa mwezi huu vinginevyo hatua zitachukuliwa dhidi yao.Akizungumza na gazeti hili wakati wa ziara ya ukaguzi kuangalia utekelezaji wa agizo la serikali juu ya ufungaji wa mfumo huo mwishoni mwa wiki, Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere alisema hatua zitachukuliwa kwa wazalishaji wote watakaokaidi agizo hilo. Akiwa jijini Mwanza, Kichere alitembelea viwanda kadhaa kikiwemo Kiwanda cha Premidis kinachotengeneza pombe kali aina ya Shimha Waragi eneo la viwanda la Nyakato.Akiwa kiwandani hapo Kichere aligundua kuwa bado kinatumia mfumo wa zamani wa karatasi na kilikuwa mbioni kukwepa ushuru Sh milioni 38.6 akamtaka mmiliki kuzilipa mara moja. “Kuanzia mwishoni mwa mwezi huu viwanda vyote vinatakiwa kufunga mfumo huu mpya kama ilivyokusudiwa na serikali la sivyo hatua kali ikiwemo kuvifunga zitachukuliwa,” alisema.Viwanda vingine vilivyotembelewa ni cha Bia cha Serengeti (SBL) na cha kutengeneza mvinyo cha Mwanza Quality Wine Ltd ambapo vyote vilikutwa vinaendelea vizuri kufanyia kazi maagizo ya serikali kusimika mfumo mpya.Meneja wa SBL, Joseph Malibe na mwenzake wa Mwanza Quality Wine Ltd, Leopold Lema walisema hawana tatizo na mfumo mpya kwani utawasaidia kuhakiki vizuri mapato yao, ikiwa ni pamoja na kuwaepusha na migogoro ya mara kwa mara kati yao na mamlaka za serikali. Akiwa mkoani Shinyanga, Kichere alitembelea viwanda vinavyozalisha pombe kali vya Canon Company Ltd na East African Spirit Ltd na alijiridhisha na usimikwaji mfumo wa kuweka stempu kodi za kielektroniki katika bidhaa za vileo vinavyozalishwa na viwanda hivyo.
3
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imewakumbusha wananchi kudai risiti sahihi kila wanapofanya manunuzi ya bidhaa, la sivyo haitasita kuwatoza faini na hata kuwashitaki mahakamani.Meneja wa TRA Mkoa wa Mwanza, Ernest Dundee alisisitiza hilo alipozungumza na HabariLeo jijini hapa juzi kuhusu wajibu wa mnunuzi wa bidhaa katika kuwezesha upatikanaji wa kodi za serikali.“Kutodai risiti sahihi wakati wa manunuzi ya bidhaa ni kushiriki kukwepa kodi, ndio maana sasa tumeanza kutoza faini ya Sh 30,000 hadi Sh milioni 1.5 kwa mtu anayebainika kukwepa wajibu huo wa kisheria,”alisema.Kwa upande mwingine, mfanyabiashara anayebainika kufanya mauzo bila kutoa risiti sahihi hutozwa faini ya Sh milioni tatu hadi milioni 4.5 na kushitakiwa mahakamani anaporudia kukwepa kodi kwa mbinu hiyo.Hatua hizo za TRA ni sehemu ya kusimamia utekelezaji wa matumizi ya mashine za kielektroniki za kutolea risiti (EFDs) wakati wa mauzo na manunuzi ya bidhaa mbalimbali.Dundee ametaja faida kuu za kutoa na kudai risiti kila yanapofanyika manunuzi ya bidhaa kuwa ni kutunza kumbukumbu za msingi za kuthibitisha bidhaa au mali na uzalendo wa kushiriki katika kuwezesha upatikanaji wa kodi halali za serikali.Faida nyingine ni kuongeza uwajibikaji ambapo kwa mfano, kumbukumbu husaidia TRA kufanya makadirio sahihi ya kodi na mlipakodi kupata haki stahiki ya kikodi ikiwemo ya unafuu unaotokana na sheria za kodi.Aidha, mfanyabiashara huweza kufanya manunuzi sahihi ya kuendeleza biashara kutokana na kumbukumbu alizonazo ikiwa ni pamoja na kuboresha biashara, kuomba mkopo wa fedha na kuweka mipango endelevu.Kutoa risiti pia kunamsaidia mfanyabiashara kuimarisha na kujiongezea fursa za kibiashara ikiwemo kupata zabuni mbalimbali kutoka kwa wateja wakubwa ambao ni serikali na taasisi zake, kampuni, mashirika yasiyo ya serikali (NGOs) na wafanyabiashara wakubwa.Makisio ya mapato ya serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 ni Sh trilioni 32.9 zikiwamo trilioni 18 zinazotarajiwa kukusanywa na TRA kutokana na kodi mbalimbali.
5
WANAWAKE wanane wa Kitanzania na wengine 16 kutoka nje ya nchi, wameokolewa kufanya biashara ya ukahaba, baada ya kudanganywa kuwa wanapelekwa nje ya nchi kwa lengo la kupatiwa kazi nzuri.Aidha, kati ya wanawake hao wanane wa Kitanzania, wawili wanawasili leo saa saba mchana wakitokea Thailand, ambako walikuwa wakifanyishwa kazi hiyo ya ukahaba. Kamishna Msaidizi Magereza aliyeko katika Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji wa Haramu wa Binadamu, Ahmed Mwendadi alisema hayo jana kwenye mafunzo ya majaji kuhusu masuala ya kupambana na usafirishaji huo haramu wa binadamu jijini Dar es Salaam.Mwendadi alisema wanawake hao wanane wa Kitanzania kati ya hao wanne walitolewa nchini India na wanne nchini Thailand, ambapo kati ya hao wanne, wawili wanafika leo mchana saa saba. “Wanaotoka nje kuja Tanzania tumewahi kuokoa wanawake 12 kutoka nchini Burundi waliokuwa wanapita kwenda Uarabuni pamoja na Wanyarwanda wanne ambao walikutwa mkoani Singida wakifanyishwa kazi za nyumbani,” alisema Mwen-dadi.Alisisitiza kuwa Sekretarieti hiyo ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu, imebaini kuwa wanawake wengi wamekuwa wakisafirishwa nje ya nchi ya Tanzania kwa ajili ya kufanyishwa kazi ya ukahaba katika nchi za India, Thailand, Malasia pamoja na Indonesia. Aliitaja mikoa inayoongoza kwa usafirishaji wa biashara hiyo ya binadamu kuwapeleka nje ya nchi kuwa ni Dar es Salaam, Tanga, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Singida na Dodoma hususan katika wilaya ya Kondoa.“Hatua tunazochukua ni kufanya utafiti ili kubaini hayo, ikiwa ni pamoja na kutoa uelewa kwa vyombo vya utekelezaji wa sheria pamoja na mbinu za kuwagundua wahanga. Pili kutoa elimu kwa umma,” alisema. Alisema wanatarajia kuanza kufanya kampeni ya nyumba kwa nyumba kwa ajili ya kutoa elimu, ikiwamo jitihada kubwa ya serikali kuzuia pasipoti za makundi, lengo likiwa ni kuzuia watu wasiingie katika biashara haramu.Alisema serikali pia imechukua hatua ya kunyang’anya leseni kampuni zote zilizosajiliwa kutafutia kazi Watanzania nje ya nchi. Alisema nchini mpaka sasa kesi 23 za biashara hiyo haramu, zinaendelea mahakamani na kesi saba zimeshatolewa hukumu. Awali, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Kupambana na Kuzuia Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu, Adatus Magere alisema takwimu halisi za matukio hayo mpaka sasa hawana japo tatizo hilo lipo.“Hili ni tatizo kubwa hapa nchini kwa sababu uhalisia unapoajiri binti kutoka kule Iringa kuja Dar es Salaam kwa tafsini ni usafirishaji wa binadamu kwani ujira unaomlipa wa kazi na pesa unayolipa hailingani na kazi anazozifanya,” alisema Magere. Alisema biashara hiyo ipo katika maeneo mawili nchini; watoto wadogo wanatolewa mikoani kuletwa katika miji mikubwa kwa ajili ya kutumikishwa katika kazi, wengi wao hawaelezwi ukweli wanakwenda kufanya nini matokeo yake wanaishia kwenye ukahaba.“Wale ambao wanasafirishwa ni waathirika wanapochukuliwa wanapewa hadhi ambayo si kweli. Wakishachukuliwa na kwenda Uarabuni, Pakistan, India, China matokeo yake wanaishia kutumika katika Danguro,” alisema. Alisema wadau wakubwa wa jambo hilo ni polisi, magereza, ustawi wa jamii, uhamiaji na majaji kwani wana mpango kazi unaoshirikisha wadau wengi katika kupambana na biashara hiyo.Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya Temeke, Karim Mushi alisema mafunzo wanayoyapata yana mchango mkubwa yatawasaidia, kwani biashara haramu inahitaji uelewa mkubwa kwa wahusika wote.Akimwakilisha Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma, Jaji wa Kanda ya Mashariki Mkoa wa Dar es Salaam, Pwani na Morogoro, Beatrice Mutungi alipongeza jitihada zinazofanywa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Kitengo cha Usafirishaji Haramu wa Biashara ya Binadamu kwa kutoa elimu kwa wasimamizi wa sheria ili kuwaongezea elimu na maarifa zaidi wa kufanya kazi kwa ufanisi.
3
NA WINFRIDA NGONYANI, DAR ES SALAAM KATIKA kile kinachodaiwa kutaka kuisuka upya timu ya Simba, kocha mkuu wa timu hiyo Mcameroon, Joseph Omog, ametaja mambo saba atakayoyazingatia kurudisha timu hiyo katika hadhi yake, MTANZANIA limegundua. Simba imejichimbia mkoani Morogoro ilikoweka kambi ya kujiandaa na michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao, inayotarajia kuanza mapema Agosti mwaka huu, ikiwa chini ya Omog akisaidiwa na Mganda, Jackson Mayanja. Omog ambaye ameingia mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi cha Msimbazi, aliwahi pia kuipa ubingwa Azam FC kwa mara ya kwanza katika msimu wa mwaka 2013/14, hivyo ameonekana wazi kuwa na uchu wa kutaka kuudhihirishia umma na wadau wa soka kwa ujumla kuwa yeye ni bora. Miongoni mwa mambo ambayo Omog amepanga kuyafanya katika kambi ya timu hiyo huko mkoani Morogoro, ni pamoja na  kuhakikisha anakinoa vema kikosi cha timu hiyo ambacho bado kinaendelea kuleta wachezaji kadhaa ili kukiongezea nguvu. Omog pia amepanga kukiandaa kikosi chake kucheza kitimu, kwa kuhakikisha kuwa wachezaji wanakuwa na ushirikiano wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuwa na juhudi binafsi hasa wanapokuwa uwanjani. Mkakati wake mwingine ni pamoja na kuwaangalia kwa umakini wa hali ya juu, wachezaji anaoletewa na kuwapima kwa kuangalia wachezaji wenye tija na si bora mchezaji jambo alilodai kuwa kwa namna moja ama nyingine litaleta ustawi katika kikosi chake. Mcameroon huyu pia amepanga kuhakikisha kuwa anakisoma kikosi cha Simba kwa kuangalia na kujifunza makosa ya nyuma ambayo Simba imekuwa ikiyafanya na kuujua vema mtandao wa uongozi wa klabu hiyo ili aweze kupendekeza nini cha kufanya. Kocha Omog analenga kuifanya Simba kuwa timu ya ushindani, akimaanisha kuifanya kuwa bora zaidi hadi kufikia hatua ya kuogopwa na timu nyingine na iweze pia kujiandaa kucheza michezo kimataifa.
4
Kerr aliyasema hayo baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kulakiwa na wajumbe wa Kamati ya Simba, Collin Frisch na Said Tully.“Nimefurahi kuja Tanzania na nawaahidi viongozi na mashabiki kuwa nitahakikisha naendeleza wachezaji chipukizi ili Simba iweze kutamba sasa na baadaye,” alisema Kerr.Kocha huyo, ambaye amerithi mikoba ya Mserbia Goran Kopunovic, amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha Simba ambapo atakuwa anasaidiwa na kiungo wa zamani wa timu hiyo, Suleman Matola.Wakati Kerr akiwasili pia alikutana na kocha mpya wa makipa Idd Salim kutoka Kenya, aliyewasili tayari kwa kazi mpya kwenye klabu ya Simba.Simba waliamua kuachana na Kopunovic na kusaka kocha mpya baada ya Mserbia huyo kuhitaji Simba imlipe kiasi cha Dola za Marekani 50,000 (Sh milioni 100) kama ada ya usajili na mshahara wake ambapo kila mwezi atakuwa analipwa dola za Marekani 14,000 (Sh milioni 28).Baada ya kushindwana kwenye malipo ndipo uongozi uliamua kumsaka kocha mpya na kumpata Kerr ambaye inasemekana atalipwa mshahara wa dola za Marekani 9,000 sawa na Sh milioni 18 kwa mwezi.Dylan Kerr mwenye umri wa miaka 47, aliwahi kuwa mchezaji, alicheza beki wa kulia kwenye klabu za Leeds United, Reading, Blackpool na nyingine nyingi za Uingereza, huku akihudumu kama kocha msaidizi kwenye timu mbalimbali katika nchi za Vietnam ambako ametoka kwenye timu ya Hai Phong F.C. ambako alimaliza mkataba 2014.
4
Winfrida Mtoi KAMA ulifikiri Simba imewekeza nguvu Ligi Kuu Tanzania Bara pekee utakuwa unakosea sana kwani, Wekundu hao wamepania kufanya vizuri pia Kombe la Shirikisho(ASFC), baada ya jana kuilaza Stand United mikwaju ya penalti 3-2 na kutinga robo fainali ya michuano hiyo. Kwakukukumbusha Simba ndiye kinara wa msimamowa Ligi Kuu, ikiwa na pointi 62, baada ya kushuka dimbani mara 24, ikishinda mara 20, sare mbili na kuchapwa mara mbili. Kabla ya mikwaju ya penalti kutumia kumpata mshindi, dakika 90 za pambano hilo lililopigwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga lilikamilika kwa sare ya bao 1-1. Katika mchezo huo, Stand inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara(FDL)ilionekana kupania kuwabwaga vigogo hao wa Msimbazi kabla ya kukubali kuchemka. Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika kwa milango ya timu zote kugoma kufunguka. Simba ilikuwa ya kwanza kufunga bao la kuongoza dakika ya 50, kwa mkwaju wa penalti, uliopigwa na kiungo, Hassan Dilinga, baada ya beki wa Stand, Antidius Ishengoma kuunawa mpira akiwa ndani ya eneo la hatari. Lakini dakika ya 67, Stand ilisawazisha kupitia kwa Miraj Salehe, aliyepata pasi ya Maulid Fadhil aliyeuwahi mpira uliomponyoka beki wa Simba, Tairone Santos akiwa katika harakati za kuokoa. Dakika ya sita, Saleh alikosa bao, baada ya  kupata pasi nzuri ilichongwa na Fadhil, lakini alipiga shuti dhaifu lililodakwa na kipa wa Simba, Beno Kakolanya. Dalika ya saba Shiza Kichuya alishindwa kuiandikia bao la kuongoza Simba licha ya kupokea pasi safi ya Meddie Kagere, baada ya kupiga shuti dhaifu lilidakwa na kipa wa Stand United, Murtala Hamad Dakika 37, Kagere alikosa bao licha ya kuwa kwenye nafasi nzuri baada ya kupokea krosi ya Kichuya na kupiga mkwaju uliotoka nje. Pamoja na kila upande kusaka mabao ya ushindi, dakika 90 za pambano hilo zilikamilika kwa sare ya bao 1-1 na ndipo mikwaju ya penalti ilipotumika. Mshambuliaji wa kimataifa wa Rwanda, Kagere ndiye wa kwanza kupiga penalti kwa upande wa Simba, lakini alikosa baada kiki yake kupanguliwa na Hamad. Bahati mbaya hiyo ilimkuta pia Ibrahim Ajib wa Simba ambaye mkwaju wake uligonga mwamba wa juu, wakati Clatous Chama, Deogratius Kanda na Hassan Dilunga walifunga kwa upande wa Wekundu hao. Stand kwa upande mwingine penalti zake   zilifungwa na Fakhi Juma na Brown Raphael, huku Miraj Saleh akikosa kwa kugongesha mwamba kama ilivyokuwa kwa Majid Kimbondile aliyepaisha na Maulid Fadhil iliyopangulia. Timu nyingine zilizotinga robo fainali ni Sahare All Stars baada ya kuifunga Panama FC  mabao 5 -2 kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, Namungo FC imeifunga Mbeya City mabao 2-1 Uwanja wa Majaliwa, Lindi. Ndanda imechomoka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Kitayosa FC kwenye Uwanja wa  Nangwanda Sijaona, Mtwara.
4
Mwandishi wetu, Tanga MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema kampeni ya elimu kwa mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) itawasaidia wafanyabiashara wanaokwepa kodi kuacha vitendo hivyo vya kuikosesha Serikali mapato. Shigela ameyasema hayo ofisini kwake alipotembelewa na maafisa wa TRAwanaofanya kampeni hiyo mkoani humo ambayo imelenga kuwaelimishawafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati.  Amesema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi pengine kwa kujua au kutokua, jambo ambalo linahitaji elimu ya uelewa ili kila mwananchi afahamu wajibu wake kwenye ulipaji wa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Akiizungumzia kampeni hiyo, Shigela ameipongeza TRA kwa kuendesha zoezi hilo katika mikoa mbalimbali na kusema litaongeza ukusanyaji wa mapato baada ya wafanyabiashara kuelimishwa na kufahamu kuwa maendeleo ya nchi yanasababishwa na ulipaji wa kodi kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, barabara, umeme na maji. Shigela amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanalipa kodi kwa hiari bila kusubiri kubugudhiwa na serikali, huku akieleza kuwa serikali itaendelea kupambana na wakwepa kodi wanaoingiza bidhaa za magendo nchini kwa kupitia bandari bubu zilizopo kandokando ya Bahari ya Hindi. “Nchi yoyote haiwezi kupiga hatua ya maendeleo bila wananchi wake kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa sababu kodi ndio kila kitu huwezi kujenga barabara kama wafanyabiashara hawataki kulipa kodi, huwezi kuimarisha huduma za afya kama hakuna kodi na pia huwezi kuimarisha mifumo ya elimu bila kodi,” alisema Shigela. Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Tanga, Specioza Owure amesema kuwa, maafisa hao wa TRA wanaofanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi, watafika maeneo mbalimbali yenye wafanyabiashara katika mkoa wa Tanga na watawaelimisha kuhusu umuhimu wa kodi na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. “Maafisa hawa wanatumia jitihada zote kuwaelimisha wafanyabiashara, tunafanya hivi ili kila mmoja afahamu wajibu wake wa kulipa kodi sambamba na kusogeza huduma za TRA karibu na wateja,” alisema Owure.Kampeni ya elimu kwa mlipakodi mkoani Tanga inatarajia kumalizika Juni 30, 2020 ambapo lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara, kusikiliza maoni na changamoto zao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati.
5
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mahusiano kati ya Serikali na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, kimila ni muhimu yakaimarishwa. Aliyasema hayo juzi wakati akipokea taarifa ya mkoa wa Iringa alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Iringa kwa ajili ya ziara ya kikazi.Waziri Mkuu alisema ni lazima uhusiano huo udumishwe katika ngazi zote kwa sababu Serikali ipo kwa ajili ya wananchi wote na inawahudumia bila ya ubaguzi. Aliwataka viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia maeneo mbalimbali nchini wahakikishe wanatekeleza majukumu yao ipasavyo na uwajibikaji wao uwe na tija.Alitaka watendaji wahakikishe ukusanyaji mapato unapewa kipaumbele katika maeneo yao. “Ukusanyaji wa mapato ni muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa kwa sababu miradi ya maendeleo kama ujenzi wa shule haiwezi kutekelezeka bila ya kukusanya mapato,” alisema. Awali akisoma taarifa ya mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi alisema mkoa huo umepewa zaidi ya sh bilioni saba kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za wilaya.Alisema fedha zilizotumika kwa ujenzi wa hospitali Manispaa ya Iringa ni asilimia 98, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa asilimia 90, Kilolo asilimia 99 na Mufindi asilimia 89.Mkuu huyo wa mkoa alisema mbali na fedha hizo za ujenzi wa hospitali, pia Serikali imetoa zaidi ya Sh bilioni tatu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya. Akizungumzia uchaguzi wa Serikali za mitaa, kiongozi huyo alisema wanaendelea na maandalizi. Mkoa wa Iringa una vijiji 360, mitaa 222 na vitongoji 2,216.
3
NA BENJAMIN MASESE – MWANZA ASKARI wa jeshi la magereza, Kibemba Warioba (27) mwenye namba B.9205 WDR amekamatwa na jeshi la polisi mkoa wa Mwanza  kwa kosa la kuanzisha Chama cha Ushirika cha Akiba cha na Mikopo (Saccos) cha info tell CCM na kuwatapeli wanachama wa Chama Cha Mapinduzi, (CCM). Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza, leo Mei 26, Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Jumanne Murilo amesema askari huyo alikamatwa jana baada ya kupokea taarifa kwa wanachama wa CCM kwamba kuna saccos ya info Tell CCM inayotoa gawio kwa wanachama wa chama hicho. “Askari huyo alikuwa anafanya kazi katika gereza la Biharamulo mkoani Kagera, kabila lake ni mzanaki, mpaka sasa tunavyozungumza  na nyinyi tayari tumewasiliana na viongozi wa jeshi la magereza na amesimamishwa kazi ili kuendelea na uchunguzi na kumfikisha mahakamani. “Shughuli hii si kwamba alikuwa anaifanya yeye mwenyewe bali na watu wengine na baadhi yao tumewakamata ambao wamewatapeli wanachama wa CCM wakiwaeleza kuwa watapata gawio zuri na maisha yao yatakuwa mazuri na bora. “Mtumishi huyu ameichafua sura ya jeshi la magereza, serikali na jina la chama cha  CCM, hatuwezi kuvumilia watu wa aina hii kuendelelea kufanya uhalifu na utepeli, tutawashughulikia na kama kuna watu wenye nia ya kujihusisha na shughuli isiyo halali ni vema wakaiacha,”amesema Kamanda Murilo. Kamanda Murilo amesema baada ya taarifa hiyo kupokelewa, askari wa Mwanza walishirikiana na askari wa Mkoa wa Kagera walifuatilia mwanzilishi wa Saccos hiyo na kufanikiwa kummkamata askari huyo wa magereza akiwa na  laini za simu tano zikiwa zimesajiliwa kwa majina tofauti tofuati. Amesema baada ya uchunguzi dhidi ya askari huyo wa magereza alikiri ndiye mhusika na tayari amewatapeli wanachama wa CCM wengi na watu wengine wa kawaida  huku akitambulisha kwa vyeo mbalimbali  vilivyopo ndani ya CCM na serikali. Hata hivyo Kamanda Murilo aliwataka wanachama wa CCM na watu wengine ambao wametapeliwa na saccos hiyo kufika katika vituo vya polisi vya polisi kutoa taarifa zao ili waweze kurejeshewa fedha zao na hata kutoa ushahidi pale mtuhumiwa atakapofikishwa mahakamani. Wakati huo huo watu 29 wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa makosa mbalimbali yakiwamo mauaji ya wavuvi, wizi, unyang’anyi na upatikanaji wa dawa za kulevya aina ya bangi na mirungi. Kamanda Murilo amesema miongoni mwa watuhumiwa hao, wapo watu wawili ambao ni wavuvi wamekamatwa kwa tuhuma za mauaji  katika kisiwa cha Ukara baada ya kuwavamia wavuvi  wenzao wawili ambapo waliwafunga kamba miguuni na mikononi na kuwatumbukiza ziwani. “Mvuvi mmoja kati ya wale waliofungwa kamba amepoteza  maisha, wavamizi wamewapora  injini ya boti, kokoro moja ya kuvulia dagaa, tanki la mafuta, simu na vitu mbalimbali vyote vikiwa na thamani zaidi ya shilingi milioni tano. Kamanda Murilo amewataja watuhumiwa wa tukio hilo ni Rernard Tungaraza, Andrew Masumbuki na wenzake Sabato Msita, Laurent Julius, Sherida Paul, Joseph Charles na Juma Lisenge ambao walikamatwa katika Kisiwa cha Goziba wakiwa wanatoroka na vitu  vya wizi. Aidha ameongeza kuwa katika operesheni ya kiukamata waalifu iliyofanywa jana ya mkoani Mwanza, polisi walifanikiwa  kuwakamata watu watano kwa kosa la kupatikana na vifaa vya kutengeneza noti za fedha bandia  za Tanzania na dola ya Marekani. Watuhumiwa hao ni  Elasui Masawe, Yohana Pastory, Mussa Abbas, George Vanace, Vanace Jeremia na  Athman Idd ambapo amesema baada ya uchunguzi watafikishwa mahakamani.
3
WASHINGTON, MAREKANI   BUNGE la Marekani linatarajia kupiga kura makubaliano yanayounga mkono bajeti itakayobakisha sehemu kubwa ya programu za misaada kwa Afrika na kutoa dola bilioni moja kukabiliana na tishio la njaa. Makubaliano hayo yalitangazwa jumatatu wiki hii baada ya wabunge kukataa mpango wa kupunguza misaada unaokusudiwa kufanywa na Rais Donald Trump anayetokea Chama cha Republican. Matokeo hayo yanatokana na kutokuwa tayari kwa wabunge waandamizi wa Republicans kukata fedha za programu hizo katika Wizara ya Mambo ya Nje na Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo Marekani (USAid). Sehemu kubwa ya wabunge wanaomuunga mkono Trump, waliopendekeza kukatwa kwa misaada walijikuta wakikosa nguvu baada ya uamuzi wa viongozi wa Republican kuingia makubaliano na wabunge wa Chama cha Democrat walio wachache kuukataa mpango wa Rais. Kutokana na uamuzi huo, Rais Trump amepata pigo katika juhudi zake za kuweka ‘Marekani Kwanza’ kwa gharama ya nchi masikini. Hata hivyo, Rais Trump amesema hana jinsi atakubaliana na mpango wa matumizi ya serikali kuu unaowasilishwa na Bunge.
2
NA MARKUS MPANGALA ABEID Karume na Julius Nyerere wanafahamika kama marais waliopendelea kucheza mchezo wa bao. Nelson Mandela alipendelea mchezo wa masumbwi, na alihusudu kukutanisha wanandondi kama Mike Tyson, Evander Holyfield na Lennox Lewis. Kwa maana hiyo, kila kiongozi anakuwa na mchezo mmoja au miwili na pengine zaidi wanayopendelea kuicheza katika muda wao wa mapumziko. Nyerere hakuonekana kupenda mchezo wa soka kama Jakaya Kikwete, ambaye pia alipendelea mchezo wa kikapu, soka na muziki wa zamani na Bongofleva. Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa hakuwa  mpenzi wa michezo, ingawa nina hakika alipendelea mchezo fulani. Ama namna Rais Vladimir Putin wa Urusi anavyopendelea mchezo wa judo na kareti, pamoja na Barrack Obama anavyopenda mchezo wa kikapu, gofu na muziki. Novemba 25, mwaka huu, dunia nzima ilipigwa butwaa baada ya kutangaziwa kifo cha jabali la mapinduzi na rais wa zamani wa Cuba, Fidel Castro. Castro alikuwa swahiba mkubwa wa serikali ya awamu ya kwanza chini ya Mwalimu Nyerere na Cuba ilikuwa rafiki mzuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kifo cha Fidel Castro kimesikitisha wengi, lakini kwa umri wake wa miaka 90, uzee ulikuwa ukimtesa zaidi. Naamini kifo chake ni mapumziko. Wengi tunafahamu Fidel alikuwa bingwa wa mapigano, urushaji risasi au matumizi ya bunduki pamoja na silaha nyingine za kivita sambamba na uongozi mahiri. Pamoja na nyakati hizo ngumu, kama binadamu, alihitaji burudani, ambapo watu wa karibu wanasema alikuwa akihusudu pia vidosho alioshirikiana nao kimapenzi. Katika simulizi mbalimbali za viongozi huwa ninapendelea kujua kiongozi wa nchi yoyote anapendelea mchezo gani. Vivyo hivyo ndivyo nilivyojiuliza kwa Fidel Castro kwamba wakati wa uhai wake alipendelea mchezo gani? Baada ya kudurusu huku na huko imeonekana wazi Fidel kuna michezo aliipenda mno, mbali ya kupendelea kuvuta sigara. Mojawapo wa michezo hiyo ni mchezo wa baseball, ambao ni maarufu mno Marekani na baadhi ya mataifa ya Amerika. Picha ya Agosti mwaka 1964 inamwonesha Fidel Castro akicheza mchezo wa baseball  mjini Havana, nchini mwake Cuba. Picha nyingine ya mwaka 2002 inamwonesha akimzuia rais wa zamani wa Marekani, Jimmy Carter, asirushe mpira wa baseball katika viwanja vilivyopo Havana. Picha nyingine inamwonesha Fidel Castro akicheza mchezo wa gofu. Huu ni mchezo maarufu mno nchini Marekani, na miongoni mwa miamba ya mchezo huo ni Tiger Woods. Kwenye picha hiyo inamwonyesha Castro akimwangalia Mwanampinduzi Ernesto Che Guevara wakati akipiga mpira wa mchezo huo walioshiriki katika kitongoji cha Colina Villareal, jijini Havana. Matukio hayo yanadhihirisha kuwa Castro hakuwa kamanda wa vita pekee, bali alipenda michezo na alimudu kuicheza kwa ufasaha. Mara baada ya kuingia katika uongozi mwaka 1959, Fidel Castro alifanya kitu kimoja muhimu; kurejesha mafunzo ya elimu ya michezo na viungo na kutengeneza mikakati na sera ya kuinua michezo. Katika hilo alifanikiwa kuibua wanamichezo, walimu, wakufunzi wa kila daraja ambao walileta mafanikio makubwa. Historia inaeleza kuwa, Cuba ni nchi ya kwanza kutoka Latini Amerika kuwa na medali nyingi za michezo ya Olimpiki. Cuba ina jumla ya medali 209; dhahabu (79) fedha (67) na shaba (70). Kwenye michuano ya Olimpiki mwaka huu pekee iliyofanyika nchini Brazil, Cuba ilijipatia medali 197 kwa ujumla. Kwamba Fidel Castro alipendelea michezo, lakini yeye binafsi alikuwa na michezo fulani aliyomudu kucheza ambayo ni kriketi, gofu na baseball. Kwenye mchezo wa soka zipo picha kadhaa zinamwonyesha Fidel akipiga mpira, lakini hakuonekani kama alikuwa anahusudu mchezo huo kama ulivyo wa gofu, kriketi na baseball, ambayo ni dhahiri ilikuwa starehe kwake. Vilevile anajulikana kama kiongozi aliyependa sana kuvuta sigara. Lakini sifa nyingine ilikuwa ni kupenda vidosho. Anatajwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na vidosho mbalimbali na kwamba ilikuwa rahisi kwake kuachana na mama yake Fidelito (Fidelito yaani Fidel mdogo). Castro amejihusisha na vidosho kadhaa kabla ya kuamua kufunga pingu za maisha kimya kimya mwaka 1980 na mkewe, Dalia Soto del Valle na kuzaa naye watoto watano wa kiume. Baadhi ya vidosho hao ni Mirta Diaz-Balart, Dalia Soto del Valle, Natalia Revuelta Celia Sanchez (komredi mwenzake, sekretari na msiri wake kwa miaka 30), Juana Vera (mwalimu  na mkalimani), Gladys (mfanyakazi wa ndege), Pilar (mkalimani), Líder Máximo kwa kuwataja wachache. Huo ni ukurasa mwingine wa Fidel Castro.
4
KIU ya Rais mstaafu Benjamin Mkapa aliyokuwa nayo wakati wa utawala wake ya kutaka utoaji wa elimu bila malipo kwa wanafunzi, kwa angalau ngazi ya elimu ya msingi, imekatwa na Rais John Magufuli ambaye ameanzisha mpango wa elimu ya msingi hadi sekondari bure.Kiu ya Rais Mkapa ya kutaka utolewaji wa elimu ya msingi bure wakati wa utawala wake, imejidhihirisha katika Kitabu chake cha “My Life, My Purpose”, ambako amesema kwake alikuwa akiona kuwa nchi yenye maendeleo ni angalau inayoweza kuwapatia wananchi wake elimu bure, maji na huduma ya afya.Alibainisha kuwa alitoa hoja hiyo akiwa kwenye Mkutano wa Nchi za Jumuiya ya Madola uliofanyika Edinburgh nchini Scotland, ambako aliwaambia kuwa kuna mambo muhimu, ambayo ni ndio ya msingi kusaidia, yakifanyika yanaongeza utu na ubora wa maisha ya watu na watu wanaweza kuonekana kama watu na kuzungumza kama watu.Alisema, “Watu kwenye mkutano huo waliangalia baada ya kusema hayo na nilikuwa ninaongea nikikumbuka kuwa Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akisema mara kwa mara kuwa maendeleo ni ya watu, mimi ninapenda dhana ya maendeleo ya nchi kama Cuba ambayo wananchi wake wanapata huduma bora na bure ya elimu, maji na afya na hayo ndio maendeleo, lakini kuona watu wakilala nje tena karibia na Ikulu ya Marekani, sasa Marekani inawezaje kuonekana kuwa ni Taifa kubwa.“Kwa Tanzania nilitaka angalau kwa kuanzia kuona kuwepo kwa elimu bure ya msingi, maji na hata huduma za afya na tunatakiwa kuwekea msisitizo kwenye hayo ndio tuseme kuwa tumeendelea, naona kwa sasa kuna hili na elimu bure linatekelezwa,” alieleza Mkapa.Alipoingia madarakani, Rais Magufuli moja kati ya mambo muhimu aliyoanza nayo ni kuhakikisha elimu bila malipo kuanzia ngazi ya shule ya msingi na sekondari inapatikana.Hatua hiyo imesaidia kuongeza kiwango cha usajili wa wanafunzi wa elimu ya msingi kwa maana ya darasa la kwanza hadi ile ya sekondari, ambapo takribani Sh bilioni 23 hutumika kila mwezi. Kwenye sekta ya afya, nako pia kuna mkakati wa ujenzi wa zahanati kila kata huku huduma za maji nazo zikizidi kuimarishwa, kwa kuboresha bajeti ya maji na kuwabana wakandarasi ili kuhakikisha maji ya uhakika na bora yanapatikana kwa wakati.Pia Mkapa katika kitabu hicho, alisema alikataa mtazamo wa watu kusema Tanzania imeendelea, kwa kutoa mfano wa ongezeko la majengo makubwa mijini, huku akibainisha kuwa alikuwa akitaka kuona kwanza maisha ya watu wa vijijini yanaimarika hasa wananchi wakiwa na maji, huduma za afya na elimu bila malipo.Hata hivyo, Mkapa alipongeza harakati za sasa za uboreshaji wa maisha ya watu wa vijijini, kwa kusema kuwa kwa sasa kuna nyumba nyingi nzuri vijijini na tena zinazovutia.Aidha, tangu aingie madarakani, Rais John Magufuli amehakikisha Wakala wa Umeme Vijijini (REA) unafikisha umeme katika kila kijiji, huku Waziri mwenye dhamana ya umeme, Dk Medard Kalemani akishinda mikoani akikimbizana na wakandarasi wa umeme ili watimize azma hiyo ya rais. Lengo la hatua hiyo ni kuhakikisha unapatikana umeme wa uhakika hadi vijijini, ambao hadi sasa umesambazwa kwa asilimia zaidi ya 60.
3
MAKUNDI manne ya vyombo vya moto aina ya pikipiki zikiwemo za waendeshaji pikipiki maarufu kama ‘bodaboda’ ndio vinaruhusiwa kushikiliwa katika vituo vya polisi.Hayo yalibainishwa jana na Waziri wa Mambo ya Nje, Kange Lugola wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalumu, Rehema Migila (CUF). Katika swali lake, mbunge huyo alieleza kuwa waendeshaji bodaboda wamekuwa wakisumbuliwa na baadhi ya pikipiki zinapokamatwa na kuhifadhiwa katika vituo vya polisi wakati vikitoka kuna baadhi ya vifaa vinakosekana.Akijibu swali hilo, Waziri Lugola alisema ni makundi manne tu ya pikipiki ndio zinaruhusiwa kushikiliwa katika vituo vya polisi na zingine zote zitakazokamatwa wahusika watatakiwa kuandikiwa faini na kulipa ndani ya siku saba. Alisema zile za makundi maalumu zinaposhikiliwa katika vituo husika kuna hati mhusika anapewa kuainisha kila kifaa chake kilichopo na wakati akirudishiwa atakagua na kama kila kitu kipo.Waziri Lugola aliyataja makundi hayo kuwa ni bodaboda zilizohusika katika uhalifu, zilizohusika katika ajali za barabarani, bodaboda zilizoibiwa ambazo hushikiliwa kama kielelezo na zile zisizokuwa na wenyewe na zilizobaki zote zikikamatwa wahusika watatakiwa kuandikiwa faini na kulipwa.Awali, katika swali lake la msingi Migila alisema vijana wengi wamejiajiri kuendesha bodaboda lakini wamekuwa wakisumbuliwa na polisi kwa kukamatwa pikipiki zao mara kwa mara na je, kwa nini pikipiki zao zinapokamatwa na kisha kupelekwa polisi, siku wanapokwenda kuzichukua baadhi ya vifaa kama betri hazipo?Akijibu swali hilo la msingi, Naibu Waziri, Mambo ya Nje, Hamad Masauni alisema Sheria ya Usalama barabarani sura ya 168 iliyorejewa mwaka 2002 inampa mamlaka askari polisi kusimamisha chombo chochote barabarani na kukikagua kubaini kama kina makosa na hatimaye kukikamata.Alisema chombo kinapokamatwa hutunzwa kituoni kwa mujibu wa mwongozo wa Jeshi la Polisi Namba 229 na kwamba inapotokea kielelezo kimeharibiwa uchunguzi hufanyika na hatua huchukuliwa kwa waliohusika na upotevu huo.
3
TIMU ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wiki iliyopita ilikata tiketi ya kucheza hatua ya pili ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar 2022 baada ya kuifunga Burundi kwa penalti 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Mchezo huo ilibidi kuamriwa kwa mikwaju ya penalti tano tano baada ya timu hizo kutoka sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Bujumbura, Burundi na ule wa marudiano Jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa. Baada ya timu hizo kucheza katika muda wa kawaida wa dakika 90 na kuwa sare kwa kufungana bao 1-1 na hata baada ya kuongezewa dakika 30 matokeo yakaendelea kuwa hayo hayo na utaratibu wa penalti ndio ukatumika kumpata mshindi wa jumla wa mchezo huo.SHANGWE KILA KONA Watanzania baada ya ushindi huo walilipuka kwa furaha huku kipa Juma Kaseja akiwa gumzo kutokana na uhodari wake wa kuokoa penalti ya kwanza ya Warundi, ambayo aliipangua.Baada ya Kaseja ku pangua penalti ile, wachezaji watatu wa Tanzania walipata penalti zao huku wapinzani wao wakiendelea kukosa na hivyo kuishia kupiga penalti tatu tu kwani hata wangepata mbili zilizobaki, wasingeweza kuwafikia Taifa Stars, ambao tayari walikuwa mbele kwa penalti 3-0. Shangwe zilitimka kila kona kuanzia uwanjani, barabarani, majumbani na kila sehemu wakifurahia timu yao kutinga hatua ya makundi ya kusaka nafasi ya kucheza kwa mara ya kwanza fainali za Kombe la Dunia, ambazo zitafanyika Qatar 2022. Wengine walishangilia wakifikiri kuwa tayari Tanzania imefuzu kucheza kwa mara ya kwanza fainali za Kombe la Dunia nchini Qatar, ukweli ni kwamba tumevuka kizingiti cha kwanza na vimebaki viwili mbele yetu kabla ya kwenda Qatar.HATUA YA AWALI Tanzania pamoja na nchi zingine 27, zilitakiwa kwanza kucheza raundi hiyo ya awali ya kufuzu kabla ya kutinga hatua ya makundi baada ya nchi yetu kuwa miongoni mwa mataifa yaliyopo katika viwango vya chini vya ubora wa soka katika Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) katika mwezi Julai.Baada ya kumalizika kwa hatua ya kwanza ya kufuzu, timu 14 zitaungana na zingine 26, ambazo hazikucheza katika hatua hiyo ya awali na kuweka katika makundi 10, ambapo kila kundi litakuwa na timu nne.KAZI BADO KUBWA Tunaweza kusema kuwa kazi ndio kwanza imeanza katika mbio hizo za kusaka tiketi ya kucheza fainali za 22 za Kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar kuanzia Novemba 21 hadi Desemba 18, 2022. Kazi ndio kwanza imeanza kwani katika hatua hiyo ya makundi, ambayo itashirikisha mataifa 40 kwa Kanda ya Afrika, ambayo yatapangwa katika makundi 10 yenye timu nne kila moja, ambapo mshindi wa kila kundi, atacheza raundi ya tatu ya kufuzu.Raundi ya tatu ya kufuzu ndio ya mwisho, ambayo itakuwa na jumla ya timu 10 na timu hizo kila moja itacheza mechi mbili, ya nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla wa mechi hizo mbili, ndio atakuwa amefuzu kwenda Qatar 2022. RATIBA YA MAKUNDI Ratiba ya makundi bila shaka itakuwa ngumu zaidi kuliko ile ya awali, ambapo Taifa Stars ilicheza dhidi ya Burundi na kuiondoa kwa penalti. Bado hatutajua katika makundi Taifa Stars ita pangwa na nani na hakuna shaka kuwa huenda ikaangukia kwa vigogo wa soka barani Afrika kama Algeria, Misri, Nigeria, Cameroon, Ivory Coast, Senegal na zingine. Sasa tunachotakiwa kufanya ni kujiweka tayari kwa kukabiliana na yeyote bila kujali ukubwa au umaarufu wao, hivyo maandalizi ya mapema na ya uhakika yanatakiwa kwa timu yetu kwa ajili ya hatua hiyo ya makundi. Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) lazima lianze maandalizi mapema kwa kushirikiana na serikali ili kuhakikisha wanapata fedha mapema kwa ajili ya maandali hayo hata ikiwezekana yafanyikie nje ya nchi. Mfano wa ugumu wa mechi hizo za kufuzu tumeona baada ya Burundi, ambayo wengi walikuwa wakiidharau, kututoa jasho hadi mshindi akapatikana kwa mikwaju ya penalti.Hivyo, tujipange vizuri tusije kuwa kapu la magoli. RAI KWA WOTE Kwa umoja wetu tunatakiwa kuungana na kushirikiana ili kuhakikisha Taifa Stars inapata kila kinachotakiwa kwa ajili ya maandalizi ya mashindano hayo ya kufuzu ili tuvuke hatua inayofuata. Hilo linawezekana kama tutahakikisha tunapata ushindi kwenye mechi zetu zote za nyumbani na kupata matokeo ya kuridhisha kwenye mechi za ugenini ili kujikusanyia pointi. Tunatakiwa kuhakikisha tunapata mechi za kutosha za kirafiki tena zile za maana (kucheza na timu zenye viwango vya juu) ili tuweze kutumia na kujua wachezaji wengine ambao hawajapata nafasi ya kucheza na pia itatusaidia kupata muunganiko mzuri kwenye timu yetu ya taifa.Rai yangu kwa Watanzania, tuungane kwa pamoja na kuipa hamasa kwa kujaza Uwanja wa Taifa kila timu yetu inapocheza kwenye uwanja huo, iwe mechi za kirafiki au za kimashindano ili kuwatia moyo wachezaji wetu. Hamasa imekuwa chachu ya ushindi katika soka mfano mzuri ni klabu ya Simba katika msimu uliopita kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika, hamasa waliopewa na mashabiki wao iliwafanya wafanye vyema hadi kufikia robo fainali ya michuano hiyo. Kikubwa TFF kwa kushirikiana na Serikali kuhakikisha wachezaji wanapata huduma bora ili kuongeza chachu ya kufanya vizuri ili kuandika historia mpya katika soka letu kwa kufuzu kucheza mashindano hayo makubwa kabisa duniani.
4
MWENYEKITI wa Kijiji cha Ewor ndeke katika kata ya Kimokokua Wilaya ya Longido, Moses Lesikar Leng’ese Ole Nasuaku, anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo kwa amri ya mkuu wa wilaya hiyo akituhumiwa kujipatia kiasi cha zaidi ya Sh milioni 135 zilizolipwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kama fidia ya kupisha usambazaji wa umeme.Akizungumza na vyombo vya habari, Mkuu wa Wilaya hiyo, Frank Mwaisumbe alisema hatua hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya wananchi wa kijiji hicho kumtuhumu Mwenyekiti wao kujipatia mamilioni ya fedha kupitia mradi wa Rea baada ya kudanganya kuwa maeneo yanayopitiwa na mradi huo ni mali yake wakati si kweli.Mwaisumbe alifafanua kuwa Mwenyekiti huyo alilipwa mara mbili akitumia majina tofauti, ambapo alilipwa kiasi cha Sh milioni 66 kwa ekari saba na Sh milioni 69 kwa ekari 10 huku akitumia majina ya Lesikar Leng’ese na Moses Leng’ese na kujipatia kiasi hicho cha fedha.Alisema kuwa kabla ya kutiwa mbaroni kwa Mwenyekiti huyo, wanakijiji saba walihojiwa, watano walithibitisha maeneo hayo ni ya kijiji huku wawili wakisema ni mali ya Mwenyekiti huyo wakidai anayamiliki tangu mwaka 2013, ingawa hatua ya upimaji maeneo ya mradi ilishapita tangu mwaka 2008.“Ni kweli tumemkamata kwa kosa la kujipatia fedha kinyume cha sheria na kosa hilo linaangukia kwenye uhujumu uchumi, nimempa siku saba arejeshe fedha hizo na baada ya hapo tutampeleka mahakamani,” alisema Mwaisumbe.Aliwataja wengine waliotumia mpango huo kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia maeneo hayo ya kijiji ambao wanatafutwa ni pamoja na Elia Shapashina Kool na Luka Sambeke Ole Mboloso.Wengine ni Mwenyekiti wa kitongoji cha Maatiani aliyetambulika kwa jina moja la Kerimboti, Sindiyo Leakui na Nengolo Sadaka wote wakazi wa Kijiji cha Ewor ndeke.Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa fedha hizo zililipwa wiki tatu zilizopita kama fidia kwa maeneo yaliyopitiwa na mradi huo wa Rea baada ya kupimwa na kuthaminishwa mwaka 2008 ambapo fedha hizo zilipaswa kuwekwa kwenye akaunti ya kijiji lakini mwenyekiti huyo na wenzake walitumia akaunti binafsi kujinufaisha.
3
VIETNAM ni moja ya nchi zilizopiga hatua kubwa ya maendeleo barani Asia. Mwaka 1986 Serikali ya Vietnam ilianzisha mageuzi makubwa ya uchumi yaliyowezesha kuitoa nchi hiyo kwenye kundi la nchi masikini yenye wastani wa kipato cha Dola za Marekani 100 kwa kila mtu hadi kufi kia kuwa nchi yenye uchumi wa kati yenye kipato cha Dola za Marekani 2,000 kwa kila mtu mwaka 2014.Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli, imevutiwa na maendeleo ya nchi hiyo ambayo imetumia muda mfupi kupunguza umasikini wa wananchi wake kwa asilimia 50.Sifa kuu ya Vietnam ni uthubutu na uwezo wa kusimamia mipango yake. Mfano mwaka 1980 nchi hiyo iliamua kuingia kwenye uzalishaji mkubwa wa kahawa. Ndani ya miaka 10 iliweza kufikia uzalishaji wa tani 300,000 kwa mwaka na hatimaye kuwa nchi inayoongoza ulimwenguni katika uzalishaji na uuzaji wa kahawa aina ya Robusta.Vilevile miaka ya 1990, Vietnam ilikuwa ikiagiza mchele kutoka nje, kufuatia hatua madhubuti walizochukua mwaka 2004 ilishika nafasi ya pili duniani katika uzalishaji wa mchele kwa kuwa na misimu mitatu ya mavuno.Mafanikio makubwa ambayo Vietnam imeyapata katika kuongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo, yamekuwa chachu ya ukuaji wa sekta ya viwanda ambayo kwa sasa ndio imeshika hatamu ya uchumi wa Vietnam.Mkakati wa Mageuzi 2011- 2020 Vietnam inatekeleza mkakati wake wa kuwezesha mageuzi ya kijamii na kiuchumi wa mwaka 2011-2020 ambao umejikita kwenye kuwapatia wananchi elimu na stadi za ufundi kwa ajili ya kufanya kazi kwenye viwanda vinavyotumia teknolojia ya kisasa na ubunifu; kuboresha taasisi zinazoshughulika na masoko; na kuendelea na ujenzi wa miundombinu.Mkakati huo unaendana na utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa nchi hiyo ambao kwa sasa umelenga kufanya mageuzi makubwa katika taasisi za kibenki ili kuwezesha wananchi kupata mitaji ya kufanya shughuli za uchumi na maendeleo; na mageuzi ya makapuni ya biashara ya Serikali ili yaweze kushindana katika uchumi wa soko ndani na nje ya nchi pasipo kutegemea ruzuku kutoka serikalini.Ni dhahiri kwamba yapo mambo ambayo Tanzania inaweza kujifunza kutoka Vietnam katika safari yake ya kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Tanzania inayo nafasi kubwa ya kuongeza uzalishaji katika mazao ya miwa, mpunga na uvuvi kwa kupitia ushirikiano na Vietnam.Vietnam ambayo mwaka 1986 ilikuwa na uchumi sawa na Tanzania hivi sasa imepiga hatua kubwa kiuchumi na hawana shida ya upungufu wa chakula kama ambavyo huwa inaweza kutokea katika baadhi ya maeneo Tanzania. Kwa mfano, ukitembelea wilaya za Igunga na Nzega, utagundua kwamba kuna mabonde mengi yanayoweza kuzalisha mpunga hata mara tatu kwa mwaka lakini hajayaendelezwa kiasi hicho.Ingawa Vietnam ilianza kulima korosho miaka ya hivi karibu kwa sasa zao hilo linaongoza katika kuipatia nchi hiyo mapato mengi toafuti na Tanzania. Nini wamefanya Vietnam? Mtafiti wa Taasisi ya Utafiti wa mambo ya Biashara na Uchumi (Repoa) Dk Blandina Kilama ambaye aliwahi kufanya utafiti wake katika maeneo yanayolima korosho nchini anabainisha kuwa Tanzania ambayo miaka ya nyuma ilisifika kwa kuwa miongoni mwa nchi zinazozalishwa kwa wingi korosho zao hilo limezidi kudidimia.Katika utafiti wake ambao aliufanya huko Tandahimba mkoani Mtwara na eneo la Binh Phuoc huko Vietam akitaka kubaini kwa nini taifa hilo la Asia limepiga hatua kubwa kimaendeleo hasa katika uzalishaji katika zao la korosho kuliko Tanzania wakati mataifa hayo yanafanana kwa sehemu kubwa, nchini Vietnam uzalishaji wa zao hilo umeongezeka kutokana na sekta hiyo kuwa na wabanguaji wengi.Anasema nchini Vietnam korosho imeanza kulimwa kuanzia miaka ya 1980 na kwa sasa ndilo zao linaloiingizia nchi fedha nyingi za kigeni kuliko ilivyo hapa nchini.Anasema iwapo kutakuwa na wabanguaji wengi nchini kama ilivyo kwa Vietnam ni wazi kuwa wakulima watakuwa na nguvu ya majadiliano ya bei kuliko ilivyo sasa na pengine serikali isingelazimika kuingilia katika ununuzi wa korosho. Wakati wa utafiti wake, Vietnam ilikuwa na wabanguaji zaidi ya 300.“Kwa hali hii mbanguaji anachotaka korosho zipatikane hivyo ni lazima wajadiliane na wakulima na kuweka bei inayoridhisha kwani wakulima wa Vietnam akiona bei sio nzuri ataacha kulima zao hilo na kugeukia kwenye kilimo cha mpira,” alisema Dk Kilama.Anasema kitendo cha Tanzania kuwa na wanunuzi wachache wa zao hilo pamoja na wabanguaji kumefanya wakulima kutokuwa na sauti hali ambayo ilifanya wanunuzi kuwa na nguvu hadi kufanya serikali ikaingilia kati miaka ya nyuma na kuweka utaratibu wa stakabadhi ghalani.Anasema Tanzania ina ardhi kubwa mara tatu ya ile ya Vietnam huku idadi ya watu Tanzania ikiwa ni milioni 45 wakati Vietnam ni milioni 85 huku asilimia 70 ya watu wake kama ilivyo kwa Tanzania wakiishi vijijini.Anasema licha ya uchache wa ardhi yao; lakini katika ekari tatu wanapanda miche 600 ya korosho wakati Tanzania katika eneo hilo kunapandwa miche 200 tu kwa wakulima wadogo wa pande zote. Kwa upande wa wakulima wa kati ambao wanalima ekari sita katika eneo hilo la ardhi, Vietnam kunapandwa miche 1,500 wakati Tanzania wakulima wa kati wanamiliki ekari 10 na wanapanda miche 300.“Utaona kuwa katika ardhi ndogo wenzetu wanapanda miche mingi wakati sisi ni michache katika ardhi kubwa tuliyo nayo,” anasema Dk Kilama wakati wa utafiti wake. Anaongeza kuwa wafanyakazi katika mashamba ya mikorosho mkulima mdogo anatumia watu sita wakati Tanzania mkulima anatumia nguvu kazi ya watu 11.Kuhusu idadi ya watu anasema idadi ya kaya ya Tanzania ni sawa na ile ya Vietnam lakini tofauti kwenye kilimo hicho ni kwamba Tanzania wakulima wenyewe wanapalilia na kuokota korosho wakati Vietnam wakati wa mazao nguvu kazi ya kuokota korosho inaongezeka.Hata kwa upande wa pembejeo Tanzania wakulima hawatumii bomba la kunyunyuzi kwa ajili ya kuuawa wadudu kwa vile wanapouza mazao yao wanakopwa hivyo inawawia vigumu kununua dawa za uhakika za kuulia wadudu. Pia anasema pembejeo yenyewe inategemea serikali kuwapelekea pembejeo ya ruzuku.Kwa upande wa Vietnam wakulima wanafyeka mti kwa kutumia mashine wakati Tanzania wanatumia mapanga na mafyekeo. Mfumo wa soko la Vietnam ni mkulima kwenda kwa mnunuzi ambaye anaenda kuibangua korosho hiyo na kuiuza nje ya nchi. Upande wa soko pia korosho ya Tanzania inauzwa ikiwa ghafi kwa Serikali ambayo inatumia mfumo wa stakabadhi ghalani ambao unalalamikiwa na wakulima kuwa hauwalipi.Lakini ni mfumo ambao ulianzishwa baada ya kuona wanunuzi wanakuwa na nguvu kuliko wakulima wenyewe. Mtaalamu huyu anasema Vietnam na Tanzania zote zilikuwa wajamaa na baada ya mageuzi mengi ya kiuchumi Tanzania iliingia kwenye soko huria na Vietnam ikaenda na mfumo wa Doi Moi ambao ulihamasisha zaidi nchi kujitosheleza kwa chakula kabla ya kuuza nje ya nchi.“Tofauti ni kwama sisi tuliporuhusu soko huria tuliliacha hadi kufanya likawa soko holela na wahisani wakawa na nguvu na sauti wakati Vietnam ilipoachana na ujamaa waliingia kwenye soko huria; lakini wakawa na mfumo ambao wahisani hawakuwa na sauti na hii imewasaidia sana,” anasema Dk Kilama. Bila shaka hatua za Rais Magufuli zinatuelekeza huko waliko wenzetu wa Vietnam.
3
Na Mwandishi Wetu, Rukwa NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, ameonya watu wakiwamo wanasiasa wanaoeneza taarifa za uongo za kuwapo baa la njaa, ni kosa na wachukuliwe hatua ikiwamo kukamatwa. Masauni amesema bado kuna watu wanajichukulia mamlaka ambayo si yao na kueneza uongo kuwa kuna njaa nchini, hilo ni kosa kwa kuwa wanaeneza propaganda ambayo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani. “Hizo ni propaganda za watu wasioitakia mema nchi hii …mtu anapofanya kosa lazima achukuliwe hatua, Jeshi la Polisi liangalieni hili,” alisema. Masauni alitoa onyo hilo wakati wa ziara yake ya siku moja aliyoifanya jana mkoani Rukwa ambako mkuu wa mkoa huo, Zelothe Steven, alimhakikishia mkoa huo hauna njaa bali una ziada ya kutosha. “Nyie wenyewe mmemsikia mkuu wa mkoa (Zelothe), amethibitisha hakuna njaa mkoani hapa, lakini si hapa tu, pia mikoa ya Mbeya na Songwe wamenithibitishia hawana njaa. “Sasa wapo wanasiasa uchwara wanaeneza propaganda kuna njaa, si mamlaka yao kutangaza kuna njaa, kueneza uongo kama huo si sawa kwa kuwa kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini, wanastahili kuchukuliwa hatua ikiwamo kukamatwa,” alisema. Naye Zelothe, alisema hali ya kiusalama katika mkoa huo ni shwari ambapo amani na utulivu umeshamiri kwa kuwa una chakula cha kutosha.
3
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019  kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na  kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi  kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na  kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza.  “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake.
5
    Na MAREGESI PAUL-DODOMA SPIKA wa Bunge, Job Ndugai, ameendelea na utaratibu wa kuhariri hotuba za Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni baada ya kufanya hivyo katika hotuba iliyosomwa jana na Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Godbless Lema. Kutokana na hali hiyo, Lema alizuiwa kusoma maeneo matatu katika hotuba yake yaliyodaiwa kukiuka kanuni za Bunge. Maeneo hayo yalihusu rushwa, utesaji wa watu pamoja na watu kupotezwa. Kuzuiwa kwa hotuba hiyo ni mwendelezo wa baadhi ya hotuba za upinzani bungeni kuzuiwa kwa kile kinachodaiwa kuwa wanakiuka kanuni za kudumu za Bunge. Hotuba ya kwanza kuzuiwa ilisomwa mwezi uliopita na Mbunge wa  Malindi, Ally Saleh (CUF) iliyohusu ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na kufuatiwa na hotuba ya Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, Tundu Lissu. Wiki iliyopita, hotuba ya Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joseph Mbilinyi (maarufu kwa jina la Sugu) nayo ilizuiwa na kuzua mvutano kati ya Sugu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu. Kutokana na hali hiyo, wiki iliyopita Spika Ndugai alikemea tabia hiyo na kuwalalamikia waandishi wa hotuba za upinzani ambao wanalipwa na Bunge, waache uandishi huo kwa sababu haiwezekani awalipe mshahara na baadaye waandike hotuba za kuushutumu muhimili huo. Katika tukio la jana, awali Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, aliliambia Bunge kwamba amepewa maelekezo na Spika, akimtaka Lema asisome baadhi ya maeneo yaliyodaiwa kukiuka kanuni za Bunge yaliyomo katika hotuba yake. Hata hivyo, katika maeneo aliyosoma, Lema alilalamikia ofisi na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), kwamba inasababisha msongamano na mateso magerezani kutokana na jinsi inavyofanya kazi kwa kutofuata sheria. “Chanzo muhimu kinachosababisha msongamano na mateso magerezani ni ofisi ya DPP, sheria mbovu, zisizozingatia utu na ucheleweshaji wa upelelezi kutoka Jeshi la Polisi. “Ofisi ya DPP tangu Serikali ya awamu ya nne iingie madarakani, imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali zenye nia ovu za kuitumia mahakama ndivyo sivyo kwa kupindisha haki kwa makusudi katika kesi mbalimbali. “Ofisi hiyo imekuwa ikizuia haki ya dhamana kwa watuhumiwa ambao hawajatiwa hatiani na mahakama kwani hudiriki kufanya hivyo hata katika makosa ambayo kisheria watuhumiwa wana haki ya kupata dhamana,” alisema Lema. Kuhusu kitengo cha usalama barabani cha Jeshi la Polisi, Lema alikilalamikia na kusema askari wake wanafanya kazi kwa mazoea kwa kuwa hawajapata mafunzo ya kazi zao kwa muda mrefu. Kutokana na hali hiyo, alisema kuna haja sasa masuala yanayohusu usalama barabarani, yakaanza kufundishwa kuanzia shule za msingi hadi katika vyuo vya elimu ya juu kutokana na umuhimu wake. “Tuna taarifa kwamba, mafunzo ya askari wa usalama barabarani, hayajafanyika kwa muda mrefu kutokana na ukosefu wa fedha na hivyo kuwafanya askari hao kufanya kazi kwa kuvizia magari ikiwa ni pamoja na kupanda mwenye miti wakiwa na kamera za tochi.
3
Mchezo huo ambao ni mwendelezo wa ligi hiyo ulichezwa juzi kwenye uwanja wa Amaan mjini hapa. Polisi katika mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ilifungwa na Black Sailor mabao 2-1.Licha ya Polisi kuanza kwa kusuasua katika ligi hiyo, lakini katika mzunguko wa pili imeonekana kubadilika tangu kurudi ulingoni kwa aliyekuwa mwalimu wao, Ali Suleiman Mtuli ambaye awali aliondolewa.Tangu kurudi kwa mwalimu huyo Polisi ambayo inashika nafasi ya pili kutoka mkiani ikiwa na pointi nane mchezo huu ni wanne na kiwango cha timu hiyo kimeonekana kubadilika kila inaposhuka uwanjani licha ya kuwa imefungwa katika michezo mitatu mfululizo.Black Sailor ambayo inafundishwa na kocha Juma Awadhi kufuatia matokeo hayo imefikisha pointi 21 na kushika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo ambayo inaongozwa na JKU yenye pointi 31, ikifuatiwa na Zimamoto yenye pointi 25 huku KVZ ikishika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 23.Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo kwa kupigwa mchezo mmoja utakaowakutanisha maafande wa KMKM na Kipanga.
4
NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM UPINZANI wa watani wa jadi, Simba na Yanga umehamia mahakamani baada ya Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji, kumpandisha kizimbani Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Musleh Al Rawah, akidaiwa kumpiga mwanaye. Mjumbe huyo wa Simba alipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Frank Moshi, alisomewa shtaka la kumjeruhi mtoto wa Manji, Mehboob Manji. Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali, Genis Tesha, alidai kuwa Al Rawah alifanya kosa hilo, Machi 8, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa uliopo Chang’ombe, baada ya kumalizika mchezo wa watani wa jadi ulioisha kwa Simba kushinda bao 1-0 dhidi ya Yanga. Tesha alidai kuwa siku hiyo ya tukio, mshtakiwa Al Rawah alimpiga teke Mehboob katika sehemu mbalimbali za mwili ukiwamo uso na kumsababishia majeraha mazito. Al Rawah ambaye ni mfanyabiashara na raia wa hapa nchini anayetetewa na Wakili Dk. Damas Ndumbaro, alikana shtaka hilo na upande wa mashtaka ukadai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na hawapingi dhamana kwa mshtakiwa. Kwa upande wa Wakili Ndumbaro, naye aliomba mteja wake apewe dhamana. Hakimu Moshi akitoa masharti ya dhamana kwa mshtakiwa huyo, alimtaka awe na mdhamini mmoja ambaye anatoka katika taasisi inayotambulika ama serikalini. Baada ya mdhamini kujitokeza, upande wa mashtaka ulifanyia uhakiki barua yake ndani ya saa moja kama ilivyoelekezwa na mahakama na mshtakiwa akaachiwa huru. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 20, mwaka huu kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi umekamilika ama la.
4
SAMARA ARENA, URUSI   MSHAMBULIAJI wa Brazil, Neymar Jr, ameivusha timu ya Taifa ya nchi hiyo hatua ya robo fainali baada ya jana kufunga bao moja kwenye ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mexico, mchezo wa hatua ya 16 ya michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Urusi. Mabao ya Brazil yalifungwa na Neymar  dakika ya 51 na Roberto Firmino dakika ya 88. Dakika ya saba, Neymar, alishindwa kuipatia Brazil bao la kuongoza akiwa katika nafasi nzuri baada ya  kipa wa  Mexico, Guillermo Ochoa, kupangua mchomo wake. Mexico ilijibu kwa kufanya shambulizi dakika ya 10, lakini beki wa Brazil, Fagner Lemos, alikuwa imara kuokoa  mpira wa hatari usilete madhara langoni mwao. Mexico ilionekana kuimudu vema Brazil dakika 15 za awali kutokana na kuokoa mipira mingi ya hatari ambayo ingeweza kuleta madhara. Pia ilifanya mashambulizi kadhaa ya kushtukiza kupitia kwa Chicharito na  Hirving Lozano, lakini kikwazo kilikuwa kwa ukuta wa Brazil uliokuwa chini ya Thiago Silva na Filipe Luis. Kwa upande mwingine, Neymar na Willian da Silva, mara kwa mara walilitia kashkashi lango la Mexico ambayo wa kiasi kikubwa ilibebwa na uhodari wa kipa wao Ochoa. Pamoja na jitihada za kila upande kutaka kuandika bao la kuongoza, dakika 45 za kipute hicho zilimalizika kwa nyavu kubaki salama bila kutikiswa. Kipindi cha pili, kasi ya mchezo huo iliongezeka kutokana na kila upande kusaka bao la kuongoza. Hata hivyo, Mexico iliendelea na mbinu yake ya kufanya mashambulizi ya kushtukiza na kuiacha Brazil ikimiliki mpira. Mbinu hii ndiyo iliyoisaidia Mexico kuichapa Ujerumani, ikimuacha mshambuliaji wao, Jesus Gallardo, karibu na eneo la wapinzani. Dakika 51, Willian aliwahadaa mabeki wa Mexico kabla ya kumdondoshea pasi makini, Neymar ambaye hakujiuliza nini cha kufanya zaidi ya kuukwamisha mpira wavuni. Bao hilo liliilazimisha Mexico kufanya mabadiliko dakika ya 55, alitoka Edison Alvarez na nafasi yake kuchukuliwa na Jonathan Dos Santos. Brazil nayo ilifanya mabadiliko dakika ya 86 kwa kumpuzisha Philippe Coutinho na nafasi yake kuchukuliwa na Roberto Firmino. Mabadiliko hayo yalikuwa na manufaa kwa Brazil kwani dakika ya 88 ilifanikiwa kuandika bao la pili na la ushindi kupitia kwa Firmino. Kiungo huyo wa Liverpool ya England alifunga bao hilo baada ya kumalizia wavuni mpira uliotemwa na Ochoa aliyepangua kiki ya Neymar.  
4
RAIS John Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watu zaidi ya 60 na majeruhi takribani 70 walioungua kwa moto baada ya lori lililokuwa na shehena ya mafuta kupata ajali na kisha kulipuka moto Mjini Morogoro.Ajali hiyo imetokea jana saa 2 asubuhi ambako lori hilo lililokuwa linatoka Dar es Salaam limepinduka jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu baada ya dereva wa lori kumkwepa mwendesha pikipiki na kisha mafuta yaliyokuwa yakimwagika kushika moto na kuunguza watu waliokuwa wanayachota.Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, Rais Magufuli ametoa pole kwa familia, ndugu, marafiki na wote waliopoteza jamaa zao katika ajali hii na pia amewaombea majeruhi wapone haraka.“Nimeumia sana kusikia idadi kubwa ya Watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali hii, natoa pole kwa wote walioguswa na vifo hivi hasa familia za marehemu wote, nawaombea marehemu wapumzike mahali pema peponi na majeruhi wote wapone haraka,” alisema Rais Magufuli na kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe kufikisha salamu zake za pole kwa familia na wote walioguswa na vifo hivyo.Aliagiza wizara zote zinazohusika kushughulikia ajali hiyo na ametaka Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili kuhakikisha majeruhi wote wanapatiwa matibabu ili kuokoa maisha yao.Aidha, Rais Magufuli alielezea kusikitishwa kwake na vitendo vya watu kuvamia magari yanayopata ajali kwa lengo la kujipatia bidhaa mbali mbali zilizobebwa na magari hayo na ametaka vitendo hivyo vikome.“Baadhi ya magari haya yanabeba mafuta ambayo ni hatari kama ilivyotokea Morogoro, yapo magari yanabeba kemikali za sumu, yapo magari yanabeba milipuko nakadhalika, nawaomba sana tuache tabia hii,” amesisitiza Rais Magufuli.
3
MPELELEZI wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, John Maruru ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa watu wanne waliodaiwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuwa waliuawa na askari polisi mkoani Kigoma, wapo hai.Alidai kuwa watu hao wanne pamoja na Mganga wa Kituo cha Afya Nguruka, watafika mahakamani hapo kwa ajili ya kutoa ushahidi katika kesi ya uchochezi inayomkabili Zitto.Maruru ambaye ni shahidi wa kwanza, alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa.Akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga, shahidi huyo alidai kuwa watu hao wanne ambao Zitto alidai kuwa walikuwa majeruhi na kupelekwa Kituo cha Afya Nguruka, na kwamba polisi waliwachukua na kuwaua si kweli kwani wapo hai.Alidai kuwa Oktoba 28, mwaka huu, Zitto akiwa katika mkutano na waandishi wa habari alitoa maneno ya uchochezi ambayo yamesababisha kuwachonganisha wananchi na Jeshi la Polisi kwamba si watumishi bali ni wauaji wa wananchi.Maruru alidai baada ya taarifa hiyo walianza kufuatilia kwa kina ikiwemo kuwasiliana na SSP Mark Njela wa Kigoma ili wapate kujua hali ikoje kama ilivyotamkwa na Zitto.“SSP Njela aliniambia kuwa mambo yaliyosemwa ni ya uongo na dhamira ni kuchonganisha kati ya jeshi na wananchi”, alidai Maruru. Pia alidai katika kufuatilia taarifa hiyo, alikwenda maeneo ya Manzese jijini Dar es Salaam na kukuta wananchi wakijadiliana kuhusu taarifa iliyotolewa na Zitto na kwamba walionesha kuchukizwa na taarifa hiyo.“Nilirudi ofisini na kuwaita makachero wazoefu na maofisa wa makosa ya mtandao ili kupitia taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na tulipeana majukumu ikiwemo kufuatilia na kukusanya ushahidi kuhusu tuhuma hizo na kuitisha mashahidi,” alisisitiza.Aliendelea kudai kuwa kauli zilizotoka kwenye nakala ya taarifa kwa vyombo vya habari ilionesha kuwa jeshi hilo ni wauaji kwani Zitto alisema; ‘Polisi wamekwenda Kituo cha Afya Nguruka na wamewachukua majeruhi wanne waliopelekwa na kuwaua.” Pia katika taarifa hiyo ilielezwa kuwa Polisi wakiwa kwenye operesheni hiyo wameua watu wengi sana.Maruru alidai kwamba maneno hayo ni ya uchochezi na yanalenga kuwachonganisha na wananchi.Shahidi huyo alidai kitengo cha makosa ya mtandao walifanikiwa kupata ushahidi wa video na walimkamata mshitakiwa na walipompekua walimkuta na taarifa kwa vyombo vya habari.Alidai baada ya kukusanya ushahidi waliwasilisha kesi hiyo mahakamani.Katika kesi hiyo, Zitto anadaiwa Oktoba 28, mwaka huu, akiwa katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Makao Mkuu ya Ofisi ya Chama cha ACT Wazalendo alitoa maneno ya uchochezi yenye kuleta hisia ya hofu na chuki.
3
SERIKALI imejipanga kuweka eneo maalumu kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vya mifuko mbadala ya plastiki. Lengo la hatua hiyo ni kukamata fursa iliyopo nchini, baada ya katazo la mifuko hiyo ya plastiki katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).Kupatikana kwa eneo hilo, kutawezesha nchi kuzalisha bidhaa hizo kwa wingi na kuuza katika soko la Afrika Mashariki, ambapo nchi wanachama walikubaliana kusitisha matumizi ya mifuko hiyo kwa lengo la kulinda mazingira.Wakati Tanzania ikitangaza kusitishwa kwa mifuko hiyo kuanzia Juni mosi mwaka huu, nchi nyingine za jumuia hiyo ikiwemo Kenya na Rwanda, tayari zimeshachukua hatua hiyo. Uganda, Burundi na Sudan Kusini zinaendelea na michakato ya kufanya uamuzi huo.Akizungumzia uwekezaji kwenye mifuko ya plastiki, Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angella Kairuki alisema katazo la serikali kuzuia mifuko ya plastiki ni fursa kubwa kwa watanzania.Alisema watahakikisha wanaweka makatazo mengi, hata kwa mifuko ya karatasi inayotoka nje ya nchi ili kulinda soko la uzalishaji wa ndani kwa wawekezaji watakaojitokeza pamoja na wajasiriamali.Alitoa ombi kwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuona fursa hiyo, kwa kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya viwanda vya mifuko ya karatasi ili kuhakikisha ifikapo Juni 1, mwaka huu, maeneo ya uwekezaji yanakuwa yapo tayari.Pia alitaka kutafuta fedha ili Watanzania kuwekeza katika fursa hiyo muhimu, kwa kutengeneza mifuko inayotokana na karatasi na teknolojia mbalimbali nyingine.Kairuki alisema inakadiriwa Watanzania wanatumia mifuko bilioni tatu. Kwa wastani Mtanzania mmoja anatumia mfuko mmoja au miwili kwa wiki.Wengine wanatumia mpaka mitano hadi kumi, hivyo soko ni kubwa na fursa ni nyingi.Alieleza kuwa wamearifiwa kuwa kuna mashine kati ya milioni mbili na tano za kutengeneza mifuko hiyo mbadala.Kwamba Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) limeeleza kuwa wanazo fursa mbalimbali watakazosaidia katika kuwekeza katika mifuko hiyo.Akizungumzia suala hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwita Waitara alikaribisha wawekezaji, kwani maeneo ya uwekezaji yako katika mikoa na halmashauri zote nchini kulingana na aina ya uwekezaji.Alisema mwekezaji anaweza kuonana na uongozi wa halmashauri husika, ambapo atakutana na wahusika kujadiliana aina ya uwekezaji na mazingira yake kisha kupatiwa eneo.Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Stella Manyanya alisema katika kukamata fursa hiyo, wanamtaka mwekezaji wa Kiwanda cha Karatasi Mgololo, kuanza kutengeneza karatasi nyepesi pia kwa ajili ya mifuko na madaftari. Alisema kiwanda hicho, kitaongeza thamani kwa kuondoa vikwazo visivyo vya lazima ili kupata mafanikio zaidi kwenye fursa hiyo .Hivi karibuni, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alisema kuanzia Juni mosi mwaka huu, itakuwa ni marufuku kutengeneza, kuingiza, kuuza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubeba bidhaa za aina yoyote na matumizi yake yatakoma ifikapo Mei 31, 2019.Alisema amemuagiza waziri anayesimamia masuala ya mazingira, ikiwemo kuzungumza na wadau wenye viwanda vya kutengeneza mifuko ya plastiki kwa ajili ya kuhakikisha jambo hili linatekelezwa kwa haraka.Wametoa fursa ya viwanda, kubadilisha teknolojia, wauzaji kuondoa mzigo uliopo, Ofisi ya Waziri wa Nchi, Makamu wa Rais itajiandaa kutumia kanuni chini ya Sheria ya Mazingira ili kulifanya katazo hili kuwa na nguvu ya kisheria.“Tunachukua hatua hii ili kulinda afya ya jamii, wanyama, mazingira na miundombinu dhidi ya athari kubwa zinazotokana na taka za plastiki,” alisema.Alibainisha kuwa serikali inatambua kwamba kuna baadhi ya bidhaa, lazima zifungwe kwenye vifungashio vya plastiki na kwamba vifungashio kwa bidhaa hizo havitapigwa marufuku.
5
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda amesema pamoja na umuhimu wa nyuki katika kujikomboa kiuchumi, bado sekta hiyo haijatiliwa mkazo ipasavyo.Pinda aliyasema hayo jijini hapa wakati wa uzinduzi wa warsha iliyowakutanisha wadau wa ufugaji wa nyuki na wataalamu wa sekta hiyo, kutathmini ya utekelezaji sera ya taifa ya ufugaji wa nyuki ya mwaka 1998, na kufanya mapitio ya sera hiyo.“Sekta ya nyuki sio ndogo kama wengi tunavyoichukulia, sisi ndio tunaoifanya sekta hii kuwa ndogo lakini ukweli ni kwamba sekta hii ni kubwa sana, tukiamua kuichukulia ‘serious’ itatutoa hapa tulipo,”alisema.Pinda alisema nyuki ni mdudu mdogo sana lakini ana umuhimu mkubwa kwenye uchavushaji wa mazao nchini ambapo takribani asilimia 70 ya uchavushaji wa mazao hufanywa na mdudu huyo.“Lakini jambo la kusikitisha ni kwamba sekta hii bado haibebwi inavyotakiwa, sijui niseme ni kutokana na muundo ndani ya wizara ambao umemfanya mdudu huyu asionekane kama ana faida nyingi sana,”alisema.Aliwataka wataalamu kuhakikisha wanawafikia wafugaji wadogo na kujua matatizo ambayo wanakutana nayo katika kazi zao na kuwasaidia katika kujua namna ya kufaidika na ufugaji wao waweze kujikomboa kiuchumi katika sekta hiyo.Naye, Mkurugenzi wa Utawala wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Lucias Mwenda, aliyekuwa akimuwakilisha Katibu Mkuu wa wizara hiyo, alisema katika kuhakikisha wanainua sekta ya nyuki waliunda kikosi kazi cha kufanya tathimini muhimu kuhusu sera hiyo.Pia aliwataka wajumbe wa warsha hiyo kutumia muda huo kupitia sera hiyo kwa umakini, kuweka michango yao kwa kuangalia maeneo ambayo bado hayasaidii kasi ya kukua kwa sekta ya nyuki ili sera itakapokamilika iweze kuleta njia na matokeo sahihi.Naye, Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki, Ezekiel Mwakalukwa alisema katika kuinua sekta hiyo waliona kuna haja ya kupitia sera ya ufugaji wa nyuki ya mwaka 1998, ili kuona namna ya kuiboresha iendane na wakati wa sasa.
3
NA WINFRIDA NGONYANI, DAR ES SALAAM ZOEZI la uchukuaji fomu za kuomba kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga, limeonekana kusuasua baada ya baadhi ya wanachama wa klabu hiyo kutojitokeza kuchukua fomu hizo. Mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Yanga ulianza rasmi jana kwa wagombea kutakiwa kwenda kuchukua fomu ya kuomba kuwania nafasi katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Juni 25 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TFF, Aloyce Komba alisema baadhi ya wanachama wamejitokeza kwa wingi katika ofisi za shirikisho hilo lakini hawakuchukua fomu hizo. “Wanachama wengi tu wamekuja leo (jana) na baadhi ya viongozi pia walituma wapambe wao, lakini hakuna hata mmoja aliyechukua fomu, wengi walisema kuwa wamekuja kuhakikisha kama kweli zimeanza kutolewa,” alibainisha Komba. Aidha, Mwenyekiti huyo aliwataka wanachama wa Yanga kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu hizo na kutoa wito kwa wale wote ambao hawajalipia kadi zao kufanya hivyo ili waweze kupiga kura kihalali. “Wanachama wajiandae, wasiolipia kadi zao wakazilipie ili waweze kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowataka, wawe hai, hii itasaidia uchaguzi kuwa huru na wa haki,” alisema. Gharama ya fomu itakuwa ni Sh 200,000 na kwa nafasi nyingine za wajumbe Sh 100,000 huku mwisho wa kurejesha fomu hizo ni Mei 31 mwaka huu.
4
HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) imeamua kurudia kuchunguza jinsi halisi ya mtoto wa mkazi wa Mbeya, Elizabeth Chengula (22) baada ya vipimo vya awali kuja na majibu ya kutatanisha.Daktari Bingwa wa Upasuaji kwa Watoto wa MNH, Zaituni Bokhary akizungumza na gazeti hili, alisema vipimo walivyopima MNH vimetoa majibu tofauti na yale ya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, jambo ambalo sio la kawaida ingawa wakati mwingine hutokea.“Kuna vipimo vinakinzana, vingine vinasema mtoto huyo ni wa kike na vingine vinasema ni wa kiume, DNA ya Mkemia inasema ana XX (mwanamke) na huyo ndio mwenye nyaraka ya kisheria, lakini vipimo vyetu kwa kutumia matundu madogo kuingia kuchunguza ndani vimeonesha XY yaani mwanamume,” alisema Dk Bokhary.Alisema Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kumfanyia mtoto huyo kipimo cha kuangalia maumbile yake ya ndani kwa kutumia matundu madogo walibaini kuwa mtoto huyo ni wa kiume, lakini majibu hayo yamekuwa ni tofauti na ya mkemia ambayo yanaonesha kuwa ni wa kike. Alisema kutokana na utata huo inabidi kujiridhisha kwa kurudia vipimo vyote ili kuwe na uhakika kabla ya kumfanyia upasuaji mtoto huyo kumrekebisha maumbile yake baada ya kubaini kama ni wa jinsi gani.“Hapa tunashughulika na kitu nyeti sana kwahiyo ni lazima uwe na uhakika kwa asilimia zote mtoto huyu ni wa jinsi gani ndipo tufanye upasuaji,” alisema. Alisema hivi karibuni ilipokuja kambi maalumu ya madaktari bingwa wa upasuaji kutoka Saudi Arabia walimuona mtoto huyo, baada ya kuoneshwa majibu ya vipimo vyake walishauri kufanya vipimo cha kuchukua kinyama kwenye kokwa zake na kupima.Alisema katika matibabu ya utata wa jinsi kama ilivyo kwa mtoto huyo, kuna timu maalumu ambayo inaundwa na madaktari bingwa wa upasuaji, madaktari bingwa wa watoto, wa kina mama pamoja na madaktari bingwa wa upande wa akili na saikolojia. Utata wa majibu kama ilivyotokea kwa mtoto huyo, Dk Zaituni alisema hali hiyo huwa inatokea, na kinachofanyika ni kuwasiliana na timu huyo tena na kukubaliana kurudia kufanya vipimo kama ambavyo inafanyika kwanzo.Ni mwaka sasa mtoto huyo na mama yake wamekaa wodini na hiyo ni kutokana na kuwa na vipimo vingi vinavyohitaji, na kutokuwa na uwezo wa kuvilipia kwa wakati. “Mtoto huyu alikuja akiwa mdogo, ana mwaka mzima sasa wodini lakini kukaa huko muda mrefu wodini ni kwa sababu mama yake hana uwezo na vipimo vingi vinahitaji fedha sio vya bure. “Kwa sababu hana uwezo wa kulipia kipimo akiandikiwa inabidi kumuombea kwa watu wa Ustawi wa Jamii kupata ridhaa ya kupima au msaada na hiyo ni mchakato mpaka aruhusiwe, akipima anaandikiwa kipimo kingine inachukua muda tena,” alisema Bokhary.
3
WANANCHI wa Jimbo la Kondoa Mjini mkoani hapa, wamemwomba mbunge wao, Edwin Sannda awasaidie wapate umeme wa Mradi wa Nishati Vijijini (REA) unaopita katika maeneo yao ili kuboresha maisha yao.Maombi hayo waliyatoa mwishoni mwa wiki katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika maeneo mbalimbali wakati wa ziara ya mbunge kukagua miradi hiyo na kuelezea namna Ilani ya CCM inavyotekelezwa. Wananchi wa mitaa ya Bolisa, Ukunku na Mulua, walimwomba mbunge wa Kondoa Mjini, Sannda kuwasaidia kupata huduma ya umeme katika mitaa yao ambayo imepitiwa na nguzo za umeme wa REA na haijapewa umeme.Akijibu maombi hayo, mbunge huyo alisema, serikali imepanga kuhakikisha kwamba wananchi wote wanapata huduma ya umeme katika jimbo hilo. Sannda alisema, mkandarasi wa kusambaza umeme katika mitaa mbalimbali katika wilaya ya Kondoa tayari amepatikana, kinachosubiriwa sasa ni kuanza kazi baada ya kumaliza kazi katika wilaya ya Chamwino na Bahi. Sannda alisema serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kutoa huduma hii na ndio maana inafanya kazi kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza kuna maeneo yalipata huduma ya umeme mengine hayakumalizika.Alisema ilianza awamu ya pili ambayo ilikamilisha sehemu iliyobakia katika awamu ya kwanza na kuanzisha miradi mipya. Aidha aliwasihi wananchi hao kuendelea kutunza vigingi vilivyowekwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kama alama za kuweka nguzo kwani maeneo mengine wananchi wamekuwa wakiviharibu na kuwapa kazi wakandarasi wanapoanza kazi. Sannda aliwataka wananchi kuendelea kufanya maandalizi ya kusuka nyaya za umeme katika nyumba zao na kuajiandaa kuweka fedha za kulipia huduma ya kuingiza umeme katika nyumba zao.Ziara ya Sannda ilifanyika katika kata zote nane za Halmashauri ya Mji Kondoa ambapo alifanya ukaguzi wa miradi mbalimbali na kufanya mikutano ya hadhara na wananchi wa maeneo hayo. Katika mikutano hiyo ya hadhara, wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka miwili. Katika ziara hiyo pia aliongozana na viongozi mbalimbali wa CCM katika Wilaya ya Kondoa na wataalamu mbalimbali kutoka katika Halmashauri ya Mji Kondoa.
3
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM BEKI wa Azam FC raia wa Ghana, Yakubu Mohamed, amesema anafahamu mshambuliaji wa Simba, John Bocco, ni hatari hivyo alilazimika kuwa makini naye ili asiwaletee madhara. Azam ililazimishwa suluhu na Simba katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa juzi kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam. Akizungumza na MTANZANIA jana, Yakubu aliisifu Simba kwa kusema ina kikosi bora na ndiyo maana kwa kutambua hilo walilazimika kucheza kwa tahadhari ili kuhakikisha hawapotezi mchezo. “Namfahamu Bocco tangu alivyokuwa anacheza hapa, ni mchezaji mzuri sana ambaye usipokuwa naye makini anaweza akaleta madhara. “Kwa kufahamu hilo nilikuwa makini kiasi cha kutosha kuhakikisha hasababishi matatizo kwa upande wetu,” alisema. Beki huyo alisema baada ya kuambulia suluhu, wanajipanga kuhakikisha wanavuna pointi tatu katika kila mchezo wao utakaofuata. “Mpira ndivyo ulivyo, unaingia uwanjani ukiwa na matarajio lakini wakati mwingine yanakuwa kinyume. “Tunasahau yaliyopita tunajipanga upya kuhakikisha tunapata matokeo mazuri  katika michezo ijayo,” alisema. Kabla ya kujiunga na Simba msimu huu, Bocco aliichezea Azam takribani miaka 10 na kuiwezesha kupata taji moja la ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
4
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM TIMU ya Ruvu Shooting imeifunga Yanga bao 1-0, katika mchezo wa kirafiki uliochezwa katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Katika mchezo huo, Ruvu Shooting walipata bao hilo katika dakika ya 22, kutokana na beki wa Yanga, Abdallah Hajji, kujifunga kwa kichwa wakati akiokoa mpira wa krosi iliyopigwa na Shalla Juma. Licha ya bao hilo, Yanga walijitahidi kusaka bao la kusawazisha bila mafanikio na hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Ruvu walikuwa mbele kwa bao hilo moja. Kipindi cha pili Yanga walikuja kwa kasi ili kusawazisha bao hilo, ambapo katika dakika ya 49, Juma Abdul alikosa bao baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa Ruvu Shooting, lakini alipiga mpira uliopaa juu ya goli. Yanga hawakuishia hapo, walizidi kuliandama lango la Ruvu Shooting, ambapo katika dakika ya 62, Emmanuel Martin alipiga shuti kali lililopaa juu ya goli. Ruvu Shooting walijibu mashambulizi hayo katika dakika ya 69, baada ya Shalla Juma kupiga shuti kali lililotoka nje. Hadi mchezo huo unamalizika, Ruvu Shooting walitoka kifua mbele baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0. Baada ya mchezo huo, Yanga leo watasafiri kuelekea Unguja na usiku watacheza na timu ya Mlandege katika Uwanja wa Amaan, kisha keshokutwa wataelekea Pemba kuweka kambi kujiandaa na mchezo wa  Ngao ya Jamii dhidi ya watani wao, Simba, utakaochezwa Agosti 23, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
4
 MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro wamepitisha Sh bilioni 64.1 kama mapendekezo ya bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2019/20.Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Judith Mahende amesema mapendekezo ya mwaka huu yamepungua kwa Sh bilioni 1.7 sawa na asilimia 2.6 ukilinganisha na Sh bilioni 65.8 za mwaka uliopita.Amesema punguzo hilo linatokana na makisio ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) kutokujumuishwa hadi mwaka wa fedha utakapoanza pia bajeti ya miradi ya maji na matumizi ya kawaida pamoja na miradi ya wafadhili haipo kwenye bajeti.Akisoma mapendekezo hayo Mahende amesema halmashauri hiyo inatarajiwa kukusanya fedha hizo kutoka katika mapato ya ndani, ruzuku ya serikali kuu na wahisani mbalimbali wa maendeleo.Amesema katika fedha hizo Sh bilioni 52.1 sawa na asilimia 81.2 ni kwa ajili ya mishahara, Sh bilioni 4.9 sawa na asilimia 7.7 ni matumizi ya kawaida na bilioni saba sawa na asilimia 11 ni miradi ya maendeleo.Amesema halmashauri inatarajiwa kukusanya Sh bilioni 3.5 kama mapato ya ndani na Sh bilioni 60 ruzuku kutoka serikali pia halmashauri imetenga Sh milioni 987 sawa na asilimia 40 ya mapato yake ya ndani katika kuchangia miradi ya maendeleo.Aidha wanatarajia kuwasilisha ombi la Sh bilioni tatu nje ya bajeti kwaajili ya miradi ikiwemo ya uendelezaji wa Hospitali ya Wilaya ya Himo, kuendesha uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na ununuzi wa gari la kubeba taka.
3
Ramadhan Hassan -Dodoma BUNGE limepitisha muswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali wa mwaka 2020, kikiwemo kifungu cha viongozi wakuu wa mihimili ya dola kutoshtakiwa wakiwa madarakani. Akiwasilisha muswada huo bungeni jana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi, alisema katika Sheria ya Masuala ya Rais, Sura ya 9, muswada unalenga kufanya marekebisho katika kifungu cha 6 ili mashauri dhidi ya Rais kwa mambo anayodaiwa kuyatenda yeye binafsi kama raia, yaliyoruhusiwa kufunguliwa dhidi yake kwa mujibu wa ibara ya 46(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yafunguliwe baada ya kutoka madarakani. Alisema kifungu cha saba kinapendekezwa kurekebishwa ili mashauri yoyote dhidi ya Rais yafunguliwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. “Lengo la marekebisho haya ni kuwa na maudhui ya dhana ya kinga dhidi ya Rais ambayo ni kulinda hadhi ya Rais na nafasi yake,” alisema Profesa Kilangi. Hata hivyo Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ilipendekeza kifungu hicho kifutwe na badala yake sheria iruhusu mtu aliyehusika katika uvunjifu wa Katiba au haki za kiraia kuwajibika katika mahakama. Akiwasilisha maoni hayo, Msemaji Mkuu wa Kambi hiyo katika Wizara ya Sheria na Katiba, Salome Makamba, alisema kifungu cha 49 cha muswada kina mapendekezo ya marekebisho ya kifungu cha sita ili mashauri dhidi ya Rais kwa mambo anayodaiwa kuyatenda yeye binafsi kama raia na ambayo yameruhusiwa kufunguliwa dhidi yake kwa mujibu wa Ibara ya 46(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yafunguliwe baada ya kutoka madarakani. “Ni dhahiri kwamba kifungu hiki kitakuwa kinakinzana na matakwa ya Katiba kwa kuwa kifungu cha 46 (2) kimeshaweka utaratibu wa namna ya kufanya. Kama kifungu hiki kitarekebishwa, kitakuwa kinakinzana na matakwa ya Ibara ya 46 (2) na kwa vyovyote vile sheria ya kawaida haitaweza kufanya kazi mbele ya Ibara ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. “Kifungu cha 7(1) cha Sheria ya Masuala ya Rais ambacho kinapendekezwa kurekebiswa ili mashauri yoyote dhidi ya Rais yafunguliwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. “Sasa haya makosa mbali ya yale yake binafsi yaliyoainishwa, ni makosa gani yatakayohitaji aunganishwe na AG ni yapi? Je, kama ni makosa yake binafsi kwa nini atumike Mwanasheria Mkuu wa Serikali? Kwa nini asimtumie mwanasheria wake binafsi? “Sababu za mapendekezo haya ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ni kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utumishi wa umma na usawa mbele ya sheria,” alisema Salome. UMILIKI WA SILAHA Vilevile, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Kilangi alisema katika Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Silaha na Risasi, Sura ya 223, muswada unakusudia kufanya marekebisho kwa kuongeza kifungu kipya cha 20 A ili kuweka katazo kwa wamiliki halali wa silaha na risasi kuhamisha silaha hizo kwa watu wasioruhusiwa kuzimiliki. Alisema lengo la marekebisho hayo ni kuhakikisha kuwa kwa wakati wote silaha na risasi zinakuwa chini ya mmiliki halali. KINGA KWA JAJI MKUU NA MAJAJI Profesa Kilangi pia alisema katika Sheria ya Uendeshaji wa Mahakama, Sura ya 237, muswada unakusudia kufanya marekebisho kwa kuongeza kifungu kipya cha 65 A kwa lengo la kuweka masharti ya kinga dhidi ya mashtaka kwa Jaji Mkuu, majaji na maofisa wengine wa mahakama katika utekelezaji wa majukumu yao ya kimahakama. MKURUGENZI WANYAMAPORI Mwanasheria Mkuu wa Serikali alisema katika Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283, inapendekezwa kufanya marekebisho katika kifungu cha 116 ili kuondoa utaratibu wa Mkurugenzi wa Wanyamapori na maofisa wengine wa wanyamapori kutaifisha mifugo kupitia utaratibu wa kufililisha makosa na badala yake utaifishaji wa mifugo ufanywe kwa amri ya mahakama. “Hatua hii itasaidia kuondoa malalamiko ya wafugaji na wananchi kwa ujumla dhidi ya watumishi husika kutokana na kutumia vibaya mamlaka hayo,” alisema Profesa Kilangi. Aidha, alisema utaratibu unaopendekezwa utaleta uwiano na mfanano katika sheria hiyo, Sheria ya Hifadhi ya Taifa, Sura ya 282, Sheria ya Misitu, Sura ya 323 na Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Sura ya 284 katika kufililisha makosa. KAMATI NA WAFUGAJI Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria na Katiba, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mohammed Mchengerwa, alisema wamebaini na kutambua jitihada za Serikali katika kuweka mazingira mazuri na rafiki kisheria kuhusu haki za wafugaji nchini, ikiwemo kufuta mamlaka za kiutendaji zenye kuamua hatima ya mifugo ya wafugaji pasipo amri ya mahakama. Mchengerwa alisema kwa kuwa yapo madhara mengi zaidi yanayoambatana na mifugo kuendelea kushikiliwa kwenye hifadhi pasipo uangalizi wa kutosha, hivyo basi, kamati inashauri Serikali kuwa elimu itolewe kwa jamii ya wafugaji wanaoishi karibu na hifadhi za taifa, kuhusu athari za mifugo kuingilia makazi ya wanyamapori. Alisema kamati pia inashauri Serikali iandae mfumo thabiti na endelevu wa kisheria na kiutendaji utakaotoa majibu ya changamoto mbalimbali zenye kuathiri jamii ya wafugaji, wakulima na ustawi wa hifadhi za taifa kwa maendeleo endelevu ya taifa. WABUNGE WATOFAUTIANA Wakichangia mjadala huo, wabunge walitofautiana katika kifungu cha Rais kutoshtakiwa pindi anapokuwa madarakani. Mbunge wa Viti Maalumu, Salome Makamba (Chadema) alisema haiwezekani kukatengenezwa kinga kwa watu ambao wanavunja sheria kwa makusudi, hivyo ni lazima washtakiwe ili haki iweze kutendeka. “Mtashtakiwa tu, hii sheria haina nguvu, haiwezekani kukatengenezwa kinga kwa watu wanaofanya mambo makusudi, nasema hivi mtashitakiwa tu,” alisema Salome. Mbunge wa Viti Maalumu, Latifa Chande (Chadema) alisema ni lazima wenye mamkala washtakiwe kwani binadamu wote ni sawa. Hata hivyo, Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM) alisema rais ni lazima aheshimiwe huku akinukuu Qur’ani na Biblia kwamba wenye mamlaka wanatakiwa kuheshimiwa. “Rais ni lazima aheshimiwe, haiwezekani aache nchi awe anaenda mahakamani,” alisema Mlinga. Mbunge wa Viti Maalum, Asha Abdallah Juma (CCM) alisema anayepaswa kushtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na sio Rais pindi anapokuwa madarakani.
3
SERIKALI imeweka mkakati ifikapo mwakani kila Mtanzania awe amepima virusi vya Ukimwi. Chini ya mkakati huo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ipo kampeni ya upimaji na kila wanapokutana wananchi zaidi ya 100, lazima liwepo eneo la kupimia kutoa fursa ya Watanzania kupima.Alisema hayo jana wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalumu, Amina Mollel (CCM) alitaka kusikia tamko la serikali juu ya mkakati wa kusaidia vijana ambao ni waathirika wakubwa wa maambukizi ya Ukimwi.Waziri Mkuu alisema tatizo la Ukimwi nchini, limekuwa likiratibiwa vizuri na serikali tangu kampeni ya mapambano ilipoanza kwa kushirikisha wizara zote zinazohusika kulinda afya. Alisema ofisi yake ndiyo inasimamia mapambano dhidi ya Ukimwi kwa kuwa ilishaunda Tume ya Kudhibiti (Tacaids) ikishirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yenye wajibu wa kusimamia afya.Majaliwa alisema pia Bunge kupitia Kamati ya Kudumu ya Ukimwi na Dawa za Kulevya imekuwa ikishirikisha na mkakati huo wa pamoja, unaowezesha sasa kupambana na maambukizi ya virusi vya Ukimwi yanayoathiri maisha ya vijana.“Mkakati sasa uliopo ni kuhakikisha Watanzania wote, tunatakiwa kupima ili kujitambua afya yetu. Malengo yetu hadi 2020 kila Mtanzania awe amepima na ndiyo sababu imewekwa kampeni ya upimaji,” alisema. Alisema wanawake ndio wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kupima. “Mimi ni balozi wa wanaume wa upimaji, tunahamasisha kwa ujumla wake,” alisema.
3
Hadi sasa Tanzania imewekeza katika ukanda huo kwa asilimia 45, huku India ikiwekeza kwa asilimia 21, China asilimia tisa na nchi nyingine mbalimbali kwa asilimia 25. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Uwekezaji, Uhamasishaji na Uwezeshaji wa EPZA, Zawadia Nanyaro jana Dar es Salaam wakati akitoa mafunzo kwa wanahabari kuhusu maeneo ya uwekezaji hapa nchini.Alisema ukanda huo unawatafuta wawekezaji kwa ajili ya kuwekeza katika viwanda ambayo yapo manufaa mbalimbali yanayoweza kupatikana kwa Taifa na hata kwa wananchi. “Lengo kubwa la uwekezaji nchini ni kusaidia katika kukuza ajira mpya, uwekezaji mpya ambao utaongeza fedha za kigeni kwa kuwa bidhaa zitakazozalishwa katika viwanda hivyo zitauzwa nje ya nchi,” alisema Zawadia na kuongeza kuwa uwekezaji huo lazima uwe mpya ndipo atakapopatiwa leseni.Alisema tangu kuanza kwa uwekezaji katika ukanda maalumu hapa nchini yapo maeneo saba ya viwanda, huku mtaji uliowekezwa katika maeneo hayo ni dola za Kimarekani bilioni 1.27 na kampuni ziko 130. Alisema mauzo ya EPZ nje ya nchi yameweza kuingiza fedha za kigeni dola milioni 794 na ajira zilizopatikana ni 31,923.Kuhusu maeneo alisema katika eneo la viwanda lilipo jijini Dar es Salaam, lina ukubwa wa ekari 65 likiwa na viwanja takriban 20 likiwa na miundombinu yote inayohitajika. Kuhusu ujenzi wa miundombinu katika maeneo hayo alisema nchi nyingine serikali zao ndio huhusika na kujenga hivyo ili kuwavutia zaidi wawekezaji.
5
APRILI 26, 2018. Ni siku ya historia kwa wakazi wa mkoa wa Dodoma na Watanzania kwa jumla. Hii ni baada ya Rais John Magufuli kuitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji la Dodoma.“Nimejaribu kuangalia majiji yaliyopo nikaona kuna Jiji la Dar es Salaam, Jiji la Tanga, Jiji la Mbeya, Jiji la Mwanza, na kwa mamlaka niliyonayo kuanzia leo natangaza Dodoma siyo Manispaa tena, bali linakuwa jiji na kuanzia leo tarehe 26 mwezi huu na mwaka huu aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa atakuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma,” anasema Rais Magufuli.Siku hiyo hiyo, Rais Magufuli anaahidi kwenda kukutana na Rais wa Benki ya Maendeleo ili kuzungumza naye kwa ajili ya kupata fedha za kufanya miradi ya maendeleo kwa bajeti ya jiji badala ya kupata fedha za miradi yenye sura ya manispaa. Huo ni mwaka 2018 ulioipandisha hadhi Dodoma na kuifanya kuingia katika urithi wa matukio ya kihistoria Tanzania.Bunge lapitishaSpika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai anakaririwa na HabariLeo akisema: “Bunge litahakikisha linatengeneza Sheria ya Tamko la Dodoma kuwa Makao Makuu ambayo haitakuwa rahisi kukanyagwa kanyagwa na kubadili.”“Haijalishi kama sheria itakuwa na ukurasa mmoja, jambo la msingi kuwe na kipengele kinachotamka Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi kisheria. Suala hili limekuwa kwenye Ilani ya CCM (Chama Cha Mapinduzi) kwa miaka mingi sana, hivyo tunataka kutunga sheria ambayo siyo tu kwamba siyo rahisi kukanyagwa kanyagwa, bali pia ambayo ni vigumu kuibadili.”Huo ndio mwaka 2018 unaoelekea ukingoni. Itakumbukwa kuwa, serikali iliwasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018 uliolenga kulifanya Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Tanzania. Kupitia kwa muswada huo kunafanya sasa kuwepo Sheria ya Tamko la Makao Makuu ya Mwaka 2018 ambayo madhumuni yake ni kutangaza Jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya Tanzania.Sheria hiyo inatambua Tamko la Aprili 26 mwaka huu la Rais John Magufuli alipotangaza Manispaa ya Dodoma ambayo ni Mji Mkuu wa Tanzania kuwa Jiji la Dodoma. Pia inatambua uamuzi wa mwaka 1973, ambapo Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere alitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa makao makuu wa chama tawala; CCM na serikali. Kutungwa kwa sheria hiyo kunaifanya azma ya serikali kuhamia Dodoma kutimia na kuwa ndoto ya kweli.Asili ya Dodoma kuwa mji wa SerikaliKumbukumbu zinaonesha kuwa safari ya serikali kuhamia Dodoma ilianza tangu mwaka 1970. Lengo la safari hii lilikuwa kuutumia mji huu ulio katikati ya nchi kuwa kituo cha kuhudumia Watanzania wote au kutoa fursa kwa wananchi kutoka pande zote nchini kupata huduma za kiserikali bila kusafiri umbali mrefu. Mwaka 1973, Serikali inaamua kuanzisha Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) na kuundwa Programu ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma, ili kukidhi vigezo muhimu vya kuwa makao makuu ya nchi.Kimsingi, historia ya serikali kuhamia katika mji huyo ni ndefu na inaanza kuonesha matunda yake kamili mwaka 2016, ikiwa ni zaidi ya miaka 40, baada ya Rais John Magufuli kuweka bayana maamuzi na nia ya kutekeleza kwa vitendo azima ya serikali kuhamia Dodoma. Rais Magufuli baada ya kuingia madarakani katika anatangaza wazi kuwa Serikali itahamia Dodoma ifikapo 2020. Hatua hiyo inaondoa sintofahamu ya muda mrefu pamoja na kuwapo juhudi za serikali za kuwezesha uhamishaji makao makuu kupitia maamuzi mbalimbali ya chama tawala, Baraza la Mawaziri, nyaraka na miongozo ya serikali na matamko ya viongozi wakuu wa kitaifa.Hadi Desemba 8 mwaka huu, takwimu zinaonesha kuwa watumishi 6,531 kati ya watumishi takribani 7,000 wa wizara zote, walikuwa wamehamia Dodoma ikiwa ni sawa na asilimia 87.5 huku kundi la mwisho la watumishi 400 lilitarajia kuhamia kabla ya mwaka huu kuisha. Awamu ya kwanza ya watumishi 1,789 walihamia Dodoma mwaka 2016 wakiongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. Kisha, ikafuata awamu ya pili kati ya Novemba, 2017 ambapo watumishi 2,130 walihamia Dodoma wakiongoza na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na tayari awamu ya tatu kati ya Machi na Juni ni watumishi 2,612.Matarajio ni hadi mwisho wa mwaka 2018 zoezi la kuhamishia watumishi Dodoma liwe limekamilika na kuendelea na utekelezaji wa majukumu ya Serikali. Aidha, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi anabainisha kuwa hakuna mtumishi aliyehamia Dodoma ambaye anaidai serikali fedha za uhamisho.Mji wa SerikaliSerikali inajenga mji wa serikali katika eneo la Mtumba kilomita 7 nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Ujenzi wa Mji wa Serikali unatekelezwa ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa kuhakikisha watumishi wa serikali Dodoma ili wafanye kazi katika mazingira mazuri na yenye miundombinu yote itayorahisisha utendaji kazi wa kila siku. Serikali imeshatoa takribani Sh bilioni 1 za awamu wa kwanza kwa ajili ya ujenzi wa ofisi kwa ziara zote na kazi hizo kupewa vyombo vya ulinzi na usalama, jambo ambalo linao. Wizara 21 zimeanza hatua za awali za ujenzi ikiwemo kusafisha maeneo yao, kuweka mipaka, kuchimba misingi, kumwaga zegi na wengine uwekaji wa nondo na matofali ili kuanzia Januari, wizara kadhaa zianze kuhamia katika eneo hilo.Akizungumza katika ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alipotembelea na kukagua ujenzi wa majengo ya ofisi za serikali katika eneo la Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma, Katibu Mkuu Ofisi hiyo, Maimuna Tarishi anasema hatua ya serikali kuhamisha ofisi zake katika eneo hilo ina tija hasa ukizingatia kuwa tayari asilimia 87.5 ya watumishi wameshahamia Dodoma.Mpango wa utekelezaji wa ujenzi huo kwa awamu ya kwanza umefikia asilimia 82 na unatarajiwa kukamilika Januari 2019 ambapo viongozi na baadhi ya watumishi wanapaswa kuwa wamehamia katika eneo hilo mapema mwakani. Azma ya serikali ni kuhakikisha inajenga majengo bora yenye kuzingatia mahitaji yote muhimu ikiwemo miundombinu ya umeme, maji safi na taka, teknolojia ya habari na mawasiliamo (Tehama), mawasiliano na barabara katika mji wa Serikali Ihumwa.BaloziUjerumani imekuwa nchi ya kwanza kufungua ofisi ndogo mjini Dodoma itakayofanya pia shughuli za kibalozi. Pia Umoja wa Mataifa umeshafungua ofisi yake ya mawasiliano jijini hapa. Rais Magufuli alikabidhi hati miliki za viwanja kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yenye makazi yake hapa nchini kwa ajili ya kujenga ofisi na makazi jijini Dodoma. Hatimiliki zilizokabidhiwa ni 62 za balozi za nchi mbalimbali na 5 ni za mashirika ya kimataifa. Kila kiwanja kina ukubwa wa ekari 5.Hivyo Serikali kuhamia Dodoma kutoka Jiji la Dar es Salaam ni tukio la kihistoria linalopaswa kuandikwa katika vitabu na kumbukumbu za nchi yetu ikiwa ni wazo lililoanzishwa na Baba wa Taifa (Nyerere) lililoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2016 Serikali ilipohamia rasmi Dodoma na “limetiwa mhuri mzito’ Aprili 26, mwaka huu Rais Magufuli alipoipandisha hadhi Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji la Dodoma.
3
NA ABDUCADO EMMANUEL, DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm, amekunwa na bao alilofunga mshambuliaji, Donald Ngoma, wakati timu hiyo ilipolazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) juzi. Katika mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ilishuhudiwa Ngoma akifunga bao hilo dakika ya 45 kwa mpira wa kubetua aliopiga baada ya kupokea krosi safi ya juu kutoka kwa beki wa kulia, Juma Abdul na kutuliza vyema kifuani kabla ya kufunga. Azam waliocheza vizuri kipindi cha pili walisawazisha bao hilo dakika ya 82 kupitia kwa mshambuliaji wao, Kipre Tchetche, aliyeingia kuchukua nafasi ya Mkenya, Allan Wanga. Yanga walishindwa kufunga penalti iliyoonekana kuwa na utata waliyopewa na mwamuzi, Abdallah Kambuzi kutoka Shinyanga baada ya kipa wa Azam, Aishi Manula kugongana na winga, Simon Msuva, lakini kiungo Thabani Kamusoko alikosa na kupanguliwa na kipa huyo. Akizungumza na MTANZANIA mara baada ya mchezo huo, Pluijm alisema Ngoma alifunga bao zuri sana na ameonyesha thamani yake iliyomfanya apendekezwe Yanga na kusajiliwa. “Bao zuri sana, ukiona namna alivyoipokea ile krosi, alivyotuliza mpira na kufunga, inatosha kudhihirisha ubora wa bao lile. Nilimpendekeza asajiliwe na ameonyesha thamani yake kwanini yupo Yanga,” alisema. Kwa bao hilo Ngoma amefikisha mabao matano sawa na mshambuliaji wa Simba, Hamis Kiiza, wakiwa wamezidiwa bao moja na Elias Maguli wa Stand United ya Shinyanga mwenye mabao sita. Akizungumzia mechi hiyo kwa ujumla, Mholanzi huyo alisema bao walilofungwa na Azam lilitokana na makosa ya mabeki wake walioshindwa kumkaba mfungaji huku akidai walitakiwa kuwa makini muda wote wa mchezo. “Nilitarajia mechi ngumu na ndivyo ilivyokuwa, Azam walicheza kwa kutumia nguvu kuliko sisi na hilo ndilo tatizo lililotukabili. Kama unapata penalti dakika tano za mwisho na ukashindwa kufunga ni tatizo pia,” alisema. Sare hiyo inaifanya Yanga kushindwa kuifunga Azam ndani ya dakika 450 sawa na mechi tano za ligi, mara ya mwisho Wanajangwani hao kuifunga ilikuwa ni Februari 23 mwaka juzi walipoichapa 1-0. Yanga ambayo imeendelea kukaa kileleni kwa pointi 16 sawa na Azam FC kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa, itashuka tena kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam keshokutwa ikiikaribisha Toto Africans ya Mwanza.
4
KWA miezi sita ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19, Serikali imekusanya Sh trilioni 12.839 ambayo ni sawa na asilimia 80 ya lengo la nusu mwaka.Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, George Simbachawene amesema, kuanzia Julai hadi Desemba mwaka 2018, serikali imekusanya kiasi hicho ambacho ni asilimia 80.4 ya makisia ya kukusanya Sh trilioni 15.974.“Kiasi hiki lilichokusanya ni sawa na asilimia 39.5 tu ya lengo la kukusanya kiasi cha Sh trilioni 32.475 kwa mwaka mzima,” amesema Mbunge huyo wa Kibakwe (CCM).Katika bajeti ya mwaka 2018/19, serikali ilipanga kukusanya Sh trilioni 32.475, kati ya fedha hiyo, Sh trilioni 20.158 yalikuwa mapato ya ndani na Sh bilioni 735.5 mapato ya halmashauri, Sh trilioni 8.905 ni mikopo na Sh trilioni 2.130 kutoka kwa washirika wa maendeleo.Simbachawene amesema kutofikiwa kwa makusanyo katika kipindi cha nusu mwaka kwa kiasi kikubwa kumechangiwa na kutopokelewa kwa wakati misaada na mikopo kutoka nje ambapo hadi kufika Desemba mwaka jana, kiasi cha Sh bilioni 878.8 kati ya Sh trilioni 2.676 kutoka kwa washirika wa maendeleo.Amesema kamati imebaini kwa mwenendo huu wa ukusanyaji wa mapato ya serikali, inaweza kufikia makusanyo yake kati ya asilimi 80 hadi 95 na hivyo kushindwa kufikia malengo ya ukusanyaji wa mapato kwa kati ya asilimia 5 hadi 15 kwa mwaka mzima.“Kamati inaona kwamba ipo haja ya kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kutafuta vyanzo vya vipya vya mapato,” alisema.Mwenendo wa matumizi Simbachawene alisema katika kipindi cha nusu mwaka, serikali ilitumia jumla ya kiasi cha Sh trilioni 12.83, kati ya Sh trilioni 20.468 zilizoidhinishwa na Bunge kwenye matumizi ya kawaida ambayo ni asilimia 62.72.Amesema pia kiasi cha Sh trilioni 4.77 ambayo sawa na asilimia 37.1 yalitumika katika kugharamia ulipaji wa deni la Taifa pamoja na riba ya madeni yaliyoivaa na kiasi cha Sh trilioni 3.311 ambazo ni asilimi 25.6 kilitumika katika kulipia mishahara.“Mwenendo huu unaonesha kuwa kiasi cha Sh trilioni 8.081 kimetumika katika ulipaji wa Deni la Taifa na Mishahara tu na kinaobakiwa ambacho ni Sh trilioni 4.749 kimetumika katika matumizi mengineyo na maendeleo.“Pamoja na hatua hii nzuri ya utolewaji wa fedha, kamati imebaini kuna baadhi ya mafungu yamepokea zaidi ya malengo yaliyopangwa katika kipindi cha nusu mwaka na pia utolewaji wa fedha kwenye matumizi mengineyo na miradi ya maendeleo sio wa kuridhisha,” alisema.Simbachawene alitoa mfano utoaji wa fedha na asilimia ya fedha walizopata kwenye mabano kuwa ni Tume ya Mahakama (asilimia 104), Msajili wa Vyama vya Siasa (asilimia 110), Kitengo cha kuzuia fedha haramu (asilimia 114), Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (asilimia 104), Tume ya Mabadiliko ya Sheria (asilimia 338), na Hazina (asilimia 286), Mhasibu Mkuu (asilimia 134) na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (asilimia 674).“Aidha, kamati imebainika kuwa mafungu ya Msajili wa Hazina na Wizara ya Maliasili yamepewa chini ya asilimia 50, hivyo kamati inashauri serikali kuangalua mtiririko wa fedha kwa mafungu husika ili kusiathiri utekelezaji wa Bajeti kwa mafungu mengine,” alieleza.Makusanyo Alisema katika kipindi cha kati ya Julai hadi Desemba, makusanyo ya mapato ya kodi yamekuwa kwa asilimia 2 kutoka Sh trilioni 7.678 hadi Sh trilioni 7.836 ukilinganisha na kipindi kama hicho mwaka 2017/18.Mapendekezo ya kamati Alisema katika mwaka 2018/19 mapato ya serikali yalitarajiwa kukua kwa asilimia 18, hivyo basi kamati inashauri serikali kufanya tathimini ya makusanyo ya mapato katika kipindi cha nusu ya pili ya mwaka ili kufikia lengo.Pia alipendekeza kwa serikali kuangalia sera na mikakati ya kuongeza mapato ya ndani hasa kwa kupanua wigo wa kodi na kubuni na kutafuta vyanzo vipya vya mapato pamoja na kuimarisha ukusanyaji wa vyanzo vilivyopo.Maoni ya wabungeMbunge wa Nkenge, Deodorus Kamala (CCM) aliishauri serikali kuangalia upya upelekaji wa fedha za maendeleo katika wizara mbalimbali.Alisema hali inaonesha kuwa fedha zinazodaidiwa hazipelekwi kulingana na ahadi na kutolea mfano kuwa katika kipindi kilichopita Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ilipata asilimia 202 huku Maliasili ikiwa haikupata kitu.“Wizara ya Viwanda na Biashara ilipata asilimia 6.9 tu ya kile kilichohaidiwa na Wizara ya Nishati imepata asilimia 10 tu,” alisema Dk Kamala.Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) amesema ni muhimu kwa wizara tatu kukaa pamoja ili kuona namna nzuri ya kuinua uchumi. Alisema ni lazima kuwe na mkakati maalumu wa kuinua sekta ya kilimo nchini ambayo imekuwa ikichangia Pato la Taifa kwa asilimia 30.“Sekta hii ni muhimu kwani pamoja na mambo mengine inatuwezesha kuwepo kwa usalama wa chakula,” alisema na kuitaka serikali umuhimu wa serikali ikabaki na mazao ya mikakati ikiwamo pamba, tumbaku na korosho.Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba alitaka suala la ukusanyaji kodi lifanywe na wataalamu wa kodi ambao wako TRA badala ya kujumuisha Takukuru na Polisi ambao hawakusomoa masuala ya kodi.
3
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira George Simbachawene ameanza kutekeleza majukumu yake kwa kuzungumza na kiongozi wake, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kwenye ofisi ndogo ya Makamu wa Rais, Dar es Salaam.Simbachawene aliteuliwa jana kuiongoza Wizara hiyo kuchukua nafasi ya January Makamba, na ameapishwa leo Ikulu jijini humo.Baada ya kuapishwa Simbachawene alikwenda ofisini akakaribishwa na Naibu wake Mussa Sima, na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Joseph Malongo.Simbachawene ni Mbunge wa Kibakwe mkoani Dodoma na hadi alipoteuliwa alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti.Baada ya Rais Magufuli kumuapisha Simbachawene aliumuagiza aondoe vikwazo katika utoaji vibali vya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ili kuongeza kasi ya uwekezaji.Dk Magufuli amesema, wawekezaji wamekuwa wakicheleweshwa kuwekeza nchini kwa sababu kutopata vibali."Sisi tunataka kuwa na viwanda vya kutosha na wawekezaji wasiwekewe vipingamizi kwa visingizo vya NEMC kwa sababu tunahitaji viwanda ikiwezekana wawekeze viwanda, vibali vya NEMC vitakuja baadaye" amesema.Rais pia amemtaka Simbachawene asimamie suala la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na awe chachu ya Muungano huo kwa kuhakikisha anashirikiana na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa majukumu yake.
3
Na BENJAMIN MASESE, MWANZA ENEO la Shule ya Msingi Kanindo, iliyopo Kata ya Kishili, limevamiwa na wakazi ambao wamejenga nyumba huku waking’oa vigingi  vya mipaka vilivyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza mwaka 2012. Uvamizi wa eneo hilo umeonekana kuanza  kufuta ndoto za mpango uliopo wa kujengwa shule ya sekondari ili kuondoa usumbufu wa wanafunzi maeneo hayo wanaosafiri zaidi ya kilomita 8 kwa malori ya mchanga na mawe kwenda  Shule ya Sekondari  Fumagila. Kitendo hicho cha wananchi kuvamia eneo hilo kimewafanya viongozi wa kata hiyo na uongozi wa shule hiyo kuwahadhari kusitisha haraka ujenzi huo, huku kukiwapo na mvutano kwamba halmashauri  ya jiji imeshindwa kutoa fidia kwa waliokuwa wamiliki wa ardhi hiyo na kuamua kuuza kwa wanaojenga sasa. Wakizungumza katika mkutano kati wa  wananchi, Diwani wa Kata ya Kishili, Thobias Ndumi na Mtendaji wa kata hiyo,  Sayenda Mvanga, walisema wameshtushwa na taarifa kutoka kamati ya shule juu ya uvamizi huo na kulazimika kutembelea eneo hilo. Kwa upande wa Mvanga, alitoa agizo kwa wakazi ambao wamejenga nyumba zao kutoziendeleza  na hata kuzibomoa wenyewe kwa kuwa eneo hilo ni la taasisi ya umma, licha ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza kutokamilisha fidia kwa wamiliki wa eneo hilo ambao wameamua kuliuza kwa wengine ambao wanajenga sasa. “Tayari tumeanza kuchukua hatua, naombeni hili tusilaumiane, hatuwezi kuona shule inavamiwa tukae kimya kwa sababu eti fidia haijatolewa, sote ni mashahidi maeneo yote ya hapa yaliyopimwa yameanza kufidiwa, tumeanza makaburi na tutaendelea kulipa kidogo kidogo kulingana na bajeti  inayotengwa,” alisema Mvanga.
3
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM UONGOZI wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), umemfukuza kazi mtumishi wake, ambaye ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, Benadetha Kemilembe kwa kosa la utovu wa nidhamu. Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi, alisema hayo jana alipozungumza wakati alipokuwa ‘akiwafunda’ watumishi wapya 57 walioajiriwa hivi karibuni na taasisi hiyo. “Sisi ni madaktari, kazi yetu inahitaji nidhamu kwa sababu tukikosea tu, tunakuwa tumepoteza maisha ya mtu, ukipangiwa zamu zingatia. “Humu ndani (jengo) kuna ‘electronic sign’, unapaswa kusaini unapoingia na kutoka, siku tukifanya ‘analysis’, tutajua tu kwa sababu itasoma iwapo ulikuwepo au hukuwepo kazini,” alisema. Alisema daktari huyo alichukuliwa hatua wiki mbili zilizopita (Desemba 29, mwaka huu) baada ya uchunguzi kubaini alikuwa ametenda kosa. “Usipokee rushwa, na juzi walikuja hapa watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), natumaini wamewaeleza kwa kina, pia zingatieni kuvaa mavazi ya staha,” alisema. Akifafanua sakata hilo, Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa Taasisi hiyo, Ghati Chacha, alisema daktari huyo alibainika kusafiri nje ya nchi bila kibali. “Hakuwepo kazini, alikuwa mtoro, kamati ya nidhamu ilikaa na kufuatilia hadi Idara ya Uhamiaji na uchunguzi ikabainika kweli alitenda kosa, tulipatiwa taarifa pale uhamiaji na ilionyesha katika siku ambazo hakuwepo, alikuwa amesafiri kwenda Addis Ababa na hakuwa ameomba kibali kama ambavyo inatakiwa,” alisema. Kuhusu ajira hizo mpya, alisema JKCI walipatiwa kibali na Serikali kuajiri watumishi 57 na kwamba walijitokeza waomba kazi 56 na nafasi moja bado haijajazwa. “Watumishi 52 ndio ambao wameripoti hadi sasa, kati yao 23 ni wanaume na 29 wanawake, nafasi moja ambayo ni ya ofisa mipango bado ipo wazi,” alisema. Mwisho   Hali ya mapacha walioungana yaimarika   Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM HALI ya kiafya ya mapacha, Maria Mwakikuti na Consolata Mwakikuti imeimarika baada ya kupatiwa matibabu ya awali katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walikolazwa kwa matibabu ya moyo. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi, alisema bado wanaendelea kuwafanyia uchunguzi. “Wanaendelea vizuri si kama walivyoletwa awali juzi tulipowapokea, bado tunawafanyia vipimo na jopo la madaktari bingwa naliongoza mimi mwenyewe. “Kwa msingi huo, naomba ndugu waandishi wa habari mtupe muda ili tukamilishe uchunguzi tunaofanya kisha tutatoa taarifa kamili juu ya kile tulichokibaini,” alisema. Profesa Janabi alisema ikiwa watoto hao watakutwa na tatizo la moyo pekee, wanao uwezo wa kuwatibu. “Japo wamefikishwa hapa kwa tatizo la moyo, lakini ikibidi tutahusisha pia madaktari bingwa wengine wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na hata Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Ubongo, Uti wa Mgongo na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) katika matibabu yao,” alisema. Mapacha hao, walioungana kuanzia sehemu ya kifua, walifikishwa usiku wa juzi katika taasisi hiyo wakitokea mkoani Iringa baada ya kuugua. Juzi, akizungumza na MTANZANIA, mlezi wa watoto hao, Fransisca Mlangwa, alisema walianza kuugua tangu Desemba 27, mwaka jana. Alisema Consolata ndiye ambaye alikuwa na hali mbaya zaidi ya Maria, ikabidi wawapeleke katika Hospitali ya Iringa. “Walikuwa wanatapika na kukohoa, ikabidi tuwawahishe hospitalini, wakahudumiwa, lakini haemoglobin yao ikawa ndogo, wakaongezewa damu na kupatiwa matibabu mengine,” alisema.
0
Na MWANDISHI WETU KAMPUNI ya Bia ya Tanzania Breweries (TBL), imepunguza watumishi wake takribani 100 ndani ya saa 24. Taarifa ambazo gazeti hili limezipata kutoka kwa watumishi wa TBL, zinadai kwamba watumishi waliopunguzwa ni wale wa kitengo cha masoko. Mtoa taarifa mmoja kutoka kwenye duru za uongozi wa TBL ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini, ameliambia gazeti hili kuwa uamuzi huo ulitekelezwa Jumatatu ya wiki hii. Alisema sababu kuu ya kupunguza wafanyakazi hao ni kulinda uchumi wa kampuni baada ya mauzo ya bidhaa kuporomoka kwa kasi katika kipindi cha mwaka jana hadi mwaka huu. Ofisa masoko mmoja wa kampuni hiyo ambaye hajakumbwa na panga la kupunguzwa kazi, alidokeza kwamba uamuzi huo unatokana na hali ya mauzo na uchumi wa kampuni kutokuwa rafiki. Aliongeza kuwa uamuzi wa Serikali wa kuzuia biashara ya pombe kali zinazofungashwa kwenye mifuko ya plastiki(viroba) umeathiri kwa kiasi kikubwa soko la bidhaa yao aina ya Konyagi. “ Wameachishwa kinyama sana, waliitwa siku ya Jumatatu na kuachishwa papo hapo(on spot), wakaambiwa wayaache magari yao na kusaini fomu ya kuondoka, miye kwa bahati nzuri  nimepona. Na hili jambo la viroba ndio limepigilia msumali wa mwisho,” alisema ofisa huyo. MTANZANIA Jumamosi lilimtafuta kwa njia ya simu, Msemaji wa Kampuni ya TBL, Georgia Mutagahwa kwa ajili ya uthibitisho wa taarifa hiyo, hakupokea simu kila ilipopigiwa lakini akatuma ujumbe mfupi kuwa kabanwa na majukumu hivyo akaomba aandikiwe ujumbe mfupi wa maandishi. Alipoandikiwa ujumbe mfupi wa maandishi juu ya madai hayo hakujibu na hata alipopigiwa tena hakupokea simu. Kuuzwa kwa TBL Kumekuwa na hali ya sintofahamu juu ya uhalisia wa madai ya kwamba Serikali imeishauza hisa na mali zake za Kampuni ya TBL kwa Kampuni ya Sab Miller ya nchini Afrika Kusini. Inaelezwa kwamba uamuzi huo uliifanya kampuni ya Sab Miller kuungana na kutengeneza faida kubwa kwa pamoja na  Kampuni ya Anheuser-Busch (AB) InBev ya nchini Ubeligiji. Dadisi za mambo zinadai kuwa serikali ilidanganywa  na hivyo kufikia uamuzi wa kuuza kampuni ya TBL mwishoni mwa utawala wa awamu ya nne. “ Kuna dalili ya kwamba Serikali ya Awamu ya nne ilidanganywa kuuza hisa zake mutalab za viwanda vya bia cha TBL  na mali nyingine kwa ujumla wake kwa lengo la kupata fedha lakini matokeo yake ni kujikaanga yenyewe kwa sababu iliuza TBL kirahisi na kukosa fedha nyingi kama ingekuwa na subira kuhusu mpango huo,” kiliwahi kudokeza chanzo kimoja toka serikalini. Duru za mambo katika mifumo ya kiuchumi zinadai kuwa katika kipindi cha mwisho wa awamu ya nne, kama serikali  ingekuwa kikwazo kwa uuzaji wa kila kitu kwa  Sab Millier ya Afrika Kusini, kungekwamisha  kuungana na Kampuni ya Kibelgiji ya Anheuser-Busch  (AB) na InBev.      Inasemekana Sab Miller inamiliki hisa zaidi ya  asilimia 57.5  za TBL  na hivyo ndio mwenye hisa nyingi zaidi ndani ya kampuni hiyo.  Wachunguzi wa biashara na uchumi wanadai kuwa serikali ilikosa uvumilivu na hivyo kuuzwa kwa hisa zake kwa bei chee. Muunganiko (merger) hutokea pale ambapo biashara au kampuni moja inamezwa na kampuni nyingine na kupoteza utambulisho wake kwa mwenye  kuimeza na hivyo shughuli za kiuchumi huwa kubwa na hunufaika kwa ukuaji huo wa shughuli kwa kuzingatia ukubwa wake (economies of scale). Taarifa zilizopo zinaonesha kuwa  AB Inbev inamlipa Sab Miller kiasi cha dola bilioni 107 na kufanya muunganiko (merger)  huo kuwa mkubwa kuliko yote duniani  kwenye vinywaji. Zipo taarifa ambazo hazipata kuthibitishwa na serikali kwamba uuzwaji wa kampuni hiyo ulifanywa kimyakimya kwa mauzo ya dola zinazokisiwa kuwa ni milioni 200 ambazo wakosoaji wa uchumi wanasema kuwa ni chenji tu kwani wakati huo TBL ilimethaminishwa kwa bei ya soko ya dola billioni mbili.
3
Muingereza huyo alisema katika nafasi hizo tano, tatu watakuwa ni washambuliaji ambao kazi yao itakuwa ni kusaidiana na washambuliaji waliopo huku wawili wakiwa ni mabeki.Akizungumza na gazeti hili, Kerr alisema pamoja na kufurahishwa na mwenendo wa kikosi chake kubadilika katika kila mchezo, lakini amegundua kina upungufu kwa nafasi hizo na analazimika kutafuta watu mbadala ili waweze kuendana na ushindani uliopo kupigania ubingwa.“Ingawa tupo nafasi ya nne, lakini bado hatujafanya vibaya ukilinganisha idadi ya pointi kati yetu na Azam FC, ambayo inaongoza ligi tatizo kubwa kwenye kikosi changu ni baadhi ya wachezaji kutojituma na kujikuta tunategemea wachezaji wachache,” alisema Kerr.Kocha huyo alisema sababu ya kuhitaji washambuliaji watatu ni kwa ajili ya kumuongezea nguvu Hamisi Kiiza, ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwenye timu hiyo katika ufungaji na anapokosekana mambo yanakuwa magumu. Alisema nafasi ya ulinzi wanataka kumtafuta mchezaji wa kati kwa ajili ya kusaidiana na Hassan Isihaka na Juuko Murshid.“Kuna wachezaji tunaendelea nao na mazungumzo kwa ajili ya kuwasajili wakati dirisha la usajili mdogo litakapofunguliwa, naamini hakuna kitakachoharibika na tutawapata nyota hao kwa ajili ya kutuongezea nguvu kupigania ubingwa msimu huu,” alisema Kerr.Pia aliuomba uongozi wa timu hiyo na mashabiki kuwa na imani naye kama mkuu wa benchi la ufundi, kwani yeye ndiye mwenye kujua uwezo wa kila mchezaji na matatizo yanayowakabili kutokana na kuwa nao muda mwingi.Alisema ingawa timu hiyo inashika nafasi ya nne kwenye msimamo, lakini bado haijafanya vibaya kama ambavyo wanafikiria na yeye ana imani na chake kinaweza kubeba ubingwa wa Tanzania Bara.
4
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk Agness Kijazi ameibuka kidedea kwa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwa kipindi cha miaka minne 2019-2022.Dk Kijazi ambaye ni mwakilishi wa kudumu Tanzania katika Shirika hilo anakuwa mwanamke wa kwanza na mjumbe wa kwanza kutoka nchi zinazoendelea kushika nafasi hiyo.Inaelezwa kuwa atakuwa na majukumu ya kumsaidia Rais kuongoza shirika hilo katika kutekeleza majukumu yenye tija kwa wanachama wake ikiwemo Tanzania. Akizungumzia ushindi wake mbele ya wapiga kura wa mkutano wa 18 wa WMO na wajumbe waalikwa, Dk Kijazi alitoa shukrani zake kwa wote waliomuamini na kumuunga mkono hadi kufika kupata nafasi hiyo na kuahidi kuitumia nafasi hiyo kwa weledi wa hali ya juu ili kufikia malengo ya shirika hilo.“Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wote waliokuwa pamoja na mimi kwa kuniunga mkono na kunichagua kwa kura zote, naahidi kuitumikia nafasi hii kwa weledi mkubwa na kuhakikisha WMO inafikia malengo yake,” alisema Dk Kijazi.Akizungumzia ushindi huo, Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Dk Atashasta Nditiye alisema ni heshima kubwa sana kwa nchi, Wizara inampongeza sana Dk Kijazi na kuamini kuwa ataiwakilisha nchi vizuriAidha alimshukuru Rais wa Tanzania kwa ushirikiano aliouonesha kwa kukubali Tanzania kuwakilishwa na Dk Kijazi kwani jitihada zake katika kuboresha sekta ya hali ya hewa kumeendelea kuiletea sifa nchi kwa ujumla Kaimu Balozi, Ubalozi wa Kuduma Umoja wa Mataifa, Geneva Robert Kahendaguza alisema kuwa ushindi wa Dk Kijazi ni kielelezo cha umadhubuti wa kidiplomasia wa Tanzania na sifa zake binafsi ikiwemo uzoefu wa muda mrefu na elimu ya ngazi ya juu katika nyanja ya sayansi ya hali ya hewa.Uchaguzi wa viongozi wa WMO hufanyika kila baada ya miaka minne kwa kuchagua viongozi mbalimbali wakiwemo Katibu Mkuu, Rais, Makamu wa Rais wa kwanza, wa pili na wa tatu, ambapo kwa mwaka huu umefanyika katika mkutano wa 18 wa shirika hilo baada ya muda wa viongozi hao kuisha.Katika uchaguzi huo, alichaguliwa Profesa Petteri Taalas kutoka Finland (Katibu Mkuu), Profesa Dk Gerhard Adrian kutoka Ujerumani (Rais), Profesa Celeste Saulo kutoka Argentina (Makamu wa kwanza wa Rais), Dk Albert Martis kutoka Curacao (Makamu wa Pili wa Rais) na Makamu wa Tatu wa Rrais, Dk Agness Kijazi kutoka Tanzania.
3
NAIBU Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kusitisha mpango wake wa kurasimisha bandari bubu zilizopo Mkoa wa Dar es Salaam.Nditiye aliyasema hayo wakati wa ziara yake wilayani Bagamoyo ya kukagua bandari bubu zilizopo. Alisema amebaini uwepo wa bandari bubu zaidi ya 19, zinazosafirisha bidhaa kwenye eneo la mwambao wa bahari lililopo wilayani humo.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, uwepo wa bandari bubu hizo ni kipenyo cha baadhi ya wafanyabiashara, kukwepa kulipa kodi kwa kutumia bandari rasmi na hivyo kupunguza mapato ya Serikali na kuihujumu nchi.Alisema uwepo wa bandari hizo, hufifisha jitihada za Serikali za kufikia uchumi wa kati na azma yake ya ujenzi wa viwanda, utoaji wa huduma za afya, elimu, maji, umeme na ujenzi wa miudombinu katika maeneo mbalimbali nchini.Nditiye aliielekeza TPA iache mara moja mpango huo wa kurasimisha bandari bubu zilizopo Mbweni na Temeke, kwa kuwa Dar es Salaam ipo bandari na itumike hiyo kwa shughuli za usafirishaji wa bidhaa na abiria.“TPA wafute mara moja mpango wao wa kurasimisha bandari bubu za Mbweni, Temeke kuwa bandari rasmi wakati kuna bandari ya Dar es Salaam... fedha zilizotengwa na TPA kwa ajili ya mpango huo lipewe jeshi la bandari ili waweze kununua vifaa kwa ajili ya kufanya doria ya kuimarisha ulinzi kwenye mwambao wa bandari,” alisema.Alisema yapo majahazi yanayofanya shughuli za usafirishaji ufukweni mwa Bahari ya Hindi kwenye mwambao wa kilomita 300 kwenye eneo la Bagamoyo. Alisema majahazi hayo yanashusha mizigo kinyemela.Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainab Kawawa alikiri uwepo wa bandari bubu zaidi ya 19 na alimweleza Nditiye kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto za uwepo wa bandari bubu. Kawawa alitaja baadhi ya bidhaa zinazovushwa kuwa ni sukari, mafuta ya kula, matairi ya magari, maziwa ya unga, vitenge, khanga na vipodozi pamoja na wahamiaji haramu.Alisema hadi sasa kuna wafungwa wapatao 203 waliopo gerezani kutokana na uwepo wa wahamiaji haramu. Alisema watumishi hao wanatumia bandari bubu zinazotokana na uwepo wa Bahari ya Hindi wilayani humo na alizitaja kuwa ni Mlingotini, Kasiki, Kaole, Magambani, Kilimani, Badeco, Msalabani, Nunge, Mtailindi, Jicho Kuu, Mto Ruvu, Razaba, Gama, Kayanjo – shamba la chumvi, Saadani, Kitongoji cha Gwaza, Changwahela na Duza.
3
.Wizara ya Viwanda na Biashara imeweka utaratibu maalumu utakaowawezesha Wafanyabiashara katika maeneo ya mipakani kutoa taarifa juu ya vikwazo, changamoto au kero za kibiashara hasa zile zisizokuwa za kikodi wanazokutana nazo. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhandisi Stella Manyanya imesema kuwa, lengo la kuweka utaratibu huo ni kuwawezesha Wafanyabiashara kupata huduma haraka kupitia Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali zinazotoa huduma mipakani.Kwa kujibu wa taarifa hiyo, kwa kuanzia, Wizara ya Viwanda na Biashara imetoa anuani maalumu za barua pepe na namba za simu za Watendaji ambazo kila Mfanyabiashara anayepata vikwazo anaweza kutoa taarifa kupitia namba hizo. Aidha, Wizara inawataka Wakuu wa Taasisi hizo walioko kwenye vituo vya mipakani kubandika orodha hiyo kwenye mbao za matangazo ili kurahisisha mawasiliano. Vikwazo visivyokuwa vya kikodi ni pamoja na rushwa ya kifedha na isiyo ya kifedha, urasimu na kutotoa miongozo ya taratibu zinazohitajika, kukosa taarifa muhimu na kutojua fursa zilizopo.Kwa upande wa Wizara ya Viwanda na Biashara, taarifa hizo zinapaswa kutumwa kwa Mratibu wa Vikwazo Visivyo vya Kiushuru ,-Aneth Simwela kupitia barua pepe tanzania@tradebarriers.org au simu namba +255622259341.Kwa changamoto za masuala ya Viwanda na Masoko, Wafanyabiashara na Wadau wanaweza kuwasilisha changamoto zao kupitia barua pepe dawatilamsaada@mit.go.tz au kuwasiliana na Andrew Shirima wa Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia namba ya simu +255713500532.
5
MFANYABIASHARA Maiko Mrina na wenzake wawili, dereva Ally Athumani na Shabani Rashidi ambaye ni mlinzi, wamepandishwa kortini kujibu mashtaka matatu likiwemo la kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh milioni 30.Mrina alisomewa mashitaka hayo akiwa amelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) jijini Dar es Salaam kwa kuwa anaumwa.Washitakiwa hao walisomewa mashitaka jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Wakili wa Serikali Mkuu, Mkude Mshanga akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon na Glory Mwenda mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Vicky Mwaikambo.Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Agosti 29, 2018 eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam, mshitakiwa Athumani akiwa mwajiriwa wa Kampuni ya China Engineering Construction Co-operation aliiba tani nane za nondo za thamani ya Sh 35,405,390 mali ya kampuni hiyo, zilizofika kwake kutokana na nafasi yake ya ajira.Kampuni ya China Engineering Construction Co-operation ndiyo inayojengwa barabara za juu katika makutano ya Ubungo (Ubungo Interchange) jijini Dar es Salaam.Katika shitaka la pili ilidaiwa kwamba kati ya Agosti 29 hadi 30, 2018 jijini Dar es Salaam, waliisababishia serikali hasara ya Sh 30,405, 390. Katika shitaka la tatu ilidaiwa kwamba Agosti 29, 2018, washitakiwa wote walitakatisha kiasi hicho cha fedha.
3
UAMUZI wa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina kudhibiti uingizaji holela wa maziwa kutoka nje ya nchi kupitia ‘Operesheni Nzagamba’ umewezesha viwanda vipya 15 vya maziwa kuanzishwa mwaka wa fedha 2018/ 2019 vinavyosindika lita 90, 400 kwa siku.Hatua hiyo imeelezwa kuwa itaongeza soko la maziwa kwa wafugaji sambamba na kufungua fursa mpya za ajira kwa Watanzania nchini. Pia imetajwa kuongeza zaidi mapato ya serikali.Operesheni Nzagamba inayofanywa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi inalinda wazalishaji wa ndani, ajira za Watanzania na mapato ya serikali.Imeelezwa wawekezaji wengi waliogopa kuwekeza nchini kutokana na utitiri wa bidhaa za maziwa kutoka nje ya nchi zilizokuwa zinaingia nchini bila vibali, bila kukaguliwa ubora na pia kulipiwa tozo na kodi za serikali.Kaimu Msaijili wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), Dk Sophia Mlote alivitaja viwanda hivyo vipya 15 vilivyoanzishwa na mikoa vilipo kwenye mabano ni Galaxy Foods and Beverage wazalishaji wa maziwa ya ‘Kilimanjaro Fresh’ chenye uwezo wa kusindika lita 75, 000 kwa siku, Machame Dairy Products kinachosindika lita 400 kwa na Bayana Milk lita 100 (Arusha).Vingine ni Dar es Salaam Zoo Farm Milk Fresh lita 6, 000 kwa siku na Gonza Milk lita 700 kwa siku (Dar es Salaam), Mzeituni Business lita 500 kwa siku (Geita), Katavi Dairy Milk Supplier (Katavi) na Nronga Dairy lita 3, 000 (Kilimanjaro).Dk Mlote alitaja vingine kuwa ni Sebadon Milk lita 500 kwa siku (Mbeya), Mazimbu Cheese lita 500 kwa siku (Morogoro), Gema Milk lita 300 kwa siku (Ruvuma), Taishi Milk lita 1,000 kwa siku na Singida Milk lita 500 (Singida), Neema Brands lita 1,000 kwa siku (Tabora) na Bidernan Dairy lita 500 kwa siku (Tanga).Meneja Mkuu Galaxy Food & Beverage Ltd wazalishaji wa maziwa ya Kilimanjaro Fresh, Irfhan Virjee aliishukuru Serikali kwa kudhibiti uingizaji holela wa bidhaa za maziwa hatua iliyochochea kuanzishwa kwa viwanda vipya.Alisema kabla ya uamuzi huo wa serikali, ilikuwa vigumu kuanzisha viwanda vya maziwa kutokana na nchi kutawaliwa na bidhaa za maziwa zilizoingizwa nchini kwa njia za panya huku zikiwa zimekwepa ukaguzi na kodi za serikali na kusababisha ushindani usio wa haki.Baadhi ya wabunge wakichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliyowasilishwa hivi karibuni bungeni mjini Dodoma walipongeza hatua zinazochukuliwa na serikali katika kuwalinda wazalishaji maziwa wa ndani ya nchi na kutaka juhudi ziendelezwe ili kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta hiyo.“Naipongeza wizara kwa kuamua kulinda viwanda vya ndani, wizara na serikali nia yake ni kukuza viwanda vya ndani. Nimeona maziwa yetu yanaanza kupata soko kwenye nchi yetu. …. endeleeni hivyo hivyo. Tuwaunge mkono wazalishaji wa maziwa. Nendeni mtafute watu wengine wanaotaka kuanzisha biashara hii ya maziwa nchini na wapeni msaada,” alisema Mbunge wa Simanjiro, James Ole Millya.Akizungumzia mafanikio hayo ya viwanda vipya vya maziwa, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina alisema Serikali haitaogopa lawama kulinda rasilimali za nchi, wawekezaji wa ndani, ajira na uvunaji mapato ya serikali.Aliwahakishia wawekezaji hao na wengine wanaotaka kuwekeza kwenye sekta hiyo kutembea kifua mbele kwani hakuna mtu yeyote atakayechezea tena soko lao kwa sasa nchini.Alisema kutokana na mipango mizuri ya wizara yake, mitamba bora yenye mimba itaendelea kupatikana kutosheleza mahitaji ya viwanda.Alisema tangu wizara ianzishe ‘Operesheni Nzagamba’ ilikubali lawama kutoka kwa baadhi ya watu na kama wasingekuwa wavumilivu, leo viwanda vipya 15 vya maziwa visingekuwepo.Alisisitiza kuwa hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na wizara hiyo hazikulenga kumwonea mtu bali zililenga kutengeneza mazingira wezeshi ya biashara hiyo hapa nchini.
5
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara maalumu ya SMZ, Haji Omar Kheir alisema hayo wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi kwa tiketi ya CUF, Saleh Nassor Juma aliyetaka kujua lini Serikali itajenga soko la kisasa ili kuepuka wafanyabiashara wa mnada wa samaki kufanya shughuli zao katika maeneo ambayo sio rasmi.Alikiri na kusema wapo wafanyabiashara wengi wa samaki wanafanya biashara katika maeneo ya nje, ikiwemo barabarani na sio maeneo rasmi yaliyowekwa.Alisema zipo sababu nyingi zinazosababisha wafanyabiashara wa samaki kufanya kazi zao katika maeneo ambayo sio rasmi, ikiwemo ufinyu wa sehemu zilizotengwa kwa kazi hiyo.“Wafanyabiashara wetu wa samaki wanafanya kazi zao katika maeneo ambayo sio rasmi, ikiwemo barabarani na kusababisha usumbufu mkubwa na kuweka mazingira ya uchafu,” alisema.Aidha alisema baadhi ya wafanyabiashara wanakwepa kufanya kazi zao za kuuza samaki katika maeneo yaliyotengwa kwa kukwepa kutoa kodi iliyowekwa na Manispaa.Alisema kujengwa kwa soko kubwa la kisasa katika eneo la Malindi kwa kiasi kikubwa kutasaidia na kuwafanya wafayabiashara hao kutambuliwa na kulipa kodi sahihi.Kheir alisema kilichojitokeza kwa sasa ni kwamba wafanyabiashara wa samaki hulazimika kupambana na askari wa Manispaa kwa sababu ya kufanya kazi zao kinyume na sheria.Alisema ujenzi wa soko la kisasa la samaki katika eneo la Malindi unatazamiwa kugharimu jumla ya Sh bilioni 14 ambazo zitatolewa na Serikali ya Japan.
5
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
Na MWANDISHI WETU -ZANZIBAR SERIKALI imesema Shirika la Ndege nchini (ATCL), litaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha inaboresha huduma za usafiri wa anga katika visiwa vya Unguja na Pemba. Akizungumza katika kikao kilichokutanisha Kamati ya Mawasiliano na Ardhi ya Baraza la Wawakilishi (BLW) na uongozi wa Shirika hilo,  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani, alisema kuwa changamoto ambazo wameziwasilisha katika kikao hicho zitafanyiwa kazi ili kuleta tija kwa pande zote mbili. “Nawahakikishia wajumbe wa kamati hii kuwa changamoto mlizonazo tutazifanyia kazi haraka kwani ATCL sasa imezaliwa upya na hivyo itahakikisha inaboresha masilahi ya kuliinua na kuliendeleza shirika ili kuweza kukidhi mahitaji ya hapa na visiwani,” alisema Ngonyani. Alisema katika kuhakikisha huduma za usafiri wa anga visiwani humo zinaimarika, tayari Serikali imeshaanza kulipa deni lililokuwa linadaiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege la Sh milioni 241 ambalo shirika hilo linadaiwa kutokana na tozo ya maegesho ya ndege na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hamza Juma, alimwomba Naibu Waziri Ngonyani kuangalia upya suala la ajira ATCL ili liweze kubeba sura ya Muungano na kuwawezesha wataalamu wenye sifa kutoka Zanzibar nao kupata nafasi hizo. “Tunaomba Shirika na baadhi ya taasisi zinazofanya kazi kwa kushabihiana na masuala ya Muungano kuzingatia utoaji wa ajira katika nafasi wanazozitangaza kwani Zanzibar ina wataalamu wenye sifa lakini hawapati fursa,” alisema Hamza. Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, Emmanuel Korosso, alisema Shirika hilo linaendelea kuimarika na kusambaza huduma katika viwanja mbalimbali vya ndege nchini licha ya kuwa na changamoto za uhaba wa marubani
3
Wametoa kilio chao wakati wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti walipotembelewa katika mashamba yao, ambako waliangua kilio kutokana na kutumia fedha nyingi katika uzalishaji, lakini sasa wakibaki njiapanda kutokana na kutojua pa kuuzia tumbaku yao.Mwenyekiti wa Kaliua Farmers Associations, Morris Rubundi alisema licha ya serikali kuivunja TTB na kuvunja uongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku (WETCU), lakini mpaka sasa hawana mwelekeo wa mahali pa kuuzia tumbaku hiyo.Alisema muungano wao wa wakulima wa kujitegemea (IF) na vyama walipewa makadirio ya kuzalisha kilo milioni 3.7, lakini wakati wakiendelea na uzalishaji, walipokea barua ya kufutwa katika uzalishaji wa tumbaku.Alisema wakulima wa kujitegemea mkoani Tabora wanazalisha tumbaku bila kutegemea mkopo wa pembejeo, kwani wao wana uwezo wa kutumia thamani ya mali zao kukopa benki yoyote nchini kuanzia Sh milioni 100.Katibu Mkuu wa Kaliua Farmers Associations, Thomas Kimogwa alisema hadi kufikia sasa ambapo tayari wanakaribia kufungua msimu wa mauzo, hawajapokea vifungashio kutoka kampuni za ununuzi hali inayowatia wasiwasi wa jinsi ya kuuza tumbaku waliyoizalisha.Alisema kumekuwepo na tuhuma nyingi kutoka Wetcu kuwa wao sio wazalishaji, bali ni walanguzi wa tumbaku, jambo ambalo halina ukweli wowote kwa kuwa lengo la Wetcu ni kuwadidimiza wakulima kwa kujali maslahi yao binafsi.Mmoja wa wakulima wa kujitegemea na mdau mkubwa wa zao la tumbaku, Juma Mlewa alisema vyama vya ushirika haviwezi kumsaidia mkulima katika kujikwamua kiuchumi kutokana na kuwa chini ya dalali wa kampuni na taasisi cha kifedha.Alisema kwa muda mrefu wakulima wa tumbaku wamekuwa masikini kutokana na kulipa madeni ya mikopo ya benki yasiyoisha huku Wetcu wakizidi kujikusanyia mabilioni ya fedha kutoka kwa wakulima hao na kuwaacha katika dimbi la umasikini.Alisema ili kufikia malengo ya kila mkulima kunufaika na kilimo cha tumbaku, kuna haja ya serikali kufuta utitiri wa vyama vya ushirika na kubaki vyama vyenye uwezo wa uazilishaji kama walivyo IF na Associations.Aidha, aliomba serikali kuunda bodi isiyokuwa na mlengo wa kisiasa na ambayo haitaegemea upande wa wowote wa kutaka kuwanyonya wakulima wa tumbaku kama bodi iliyokuwepo hivi sasa ilijali kujipatia fedha kwa kuwanyima haki walengwa wa zao hilo.
5
Na FLORENCE SANAWA-MTWARA ULAJI wa panya umekuwa ukiwashangaza wengi huku wengine wakistaajabu juu ya ulaji wa mbwa, konokono, vyura, kenge na chatu. Viumbe hivi huliwa katika maeneo mengi duniani na hata kwa baadhi ya makabila nchini huvitumia kama kitoweo hali ambayo hufanya wengine kustaajabu pale wanapoona makabila hayo yakila. Kwa Mkoa wa Mtwara baadhi ya watu wamekuwa wakila panya, vyura na kenge. Utegaji na uuzaji wa panya umekuwa ukiwanufaisha watu wengi katika Kijiji cha Chikoweti, Kitongoji cha Mbuyuni wilayani Masasi mkoani Mtwara. Kijiji hicho kilichoko Kaskazini mwa mji wa Masasi kinakaliwa zaidi na watu wa kabila la Kimakua ambao wamekuwa na historia ya kutumia panya katika maisha yao ya kila siku kama kitoweo muhimu katika mlo.   KWANINI PANYA? “Ukiangalia kihistoria, uhaba wa samaki ndio ulitufanya tuanze kutega panya kama kitoweo, wanatusaidia kwa kuwa hawana msimu. “Panya anayeliwa huwa ni mweupe yaani ana manyoya meupe, wengi hudhani kuwa panya anayeliwa ni yule wa majumbani lakini yule hapaswi kuliwa kwa kuwa anakula vitu vingi huenda akawa na sumu mwilini,” anasema Edgar Mpupua ambaye ni maarufu kwa uwindaji, utengenezaji wa mitego na uuzaji wa panya. Naye Petro Kaonje mkazi wa Kijiji cha Chikoweti anasema ladha ya panya ni tofauti na nyama alizowahi kula ndio maana haachi kula kitoweo hicho. “Unajua unaweza kumuangalia ukamdharau lakini panya ni mtamu, sisi tunaoishi huku hatuna mabwawa wala mito ndio maana panya wanalika kutokana na uhaba wa samaki kijijini kwetu. “Sisi Wamakuwa, Wayao na Wamakonde tunapenda kula panya, hii ni asili yetu huwezi kuikana kwa kuona aibu. “Mbona wenzetu Wachina wanakula hadi mende lakini wanafurahia tu maisha, panya ni kitoweo  na ambacho kinapendwa,” anasema Kaonje na kuongeza: “Panya wanaoliwa sisi tunawafahamu na wasioliwa hatuhangaiki nao, tunapomkamata tunamchoma kisha tunakula na wali ama ugali ile ni mboga nzuri. Naye Samwel Mbaga anasema yeye si panya tu, bali pia anakula kenge, vyura na wanyama wengine ambao humpa burudani zaidi. Anasema ulaji wa kenge umekuwa ukimpa burudani zaidi kutokana na kazi kubwa ya kumpa panya hivyo kuwa rahisi kwake kumpata kenge. Kwa upande wake Martha Mkuti anasema ulaji wa panya ni wa mazoea kutokana na kutokuwa na kitoweo mbadala katika maeneo wanayoishi. “Ni kweli ladha ya panya ni kama samaki ndio maana tunaridhika kula, wapo watu wanaunga kwa nazi, ni watamu mno na wengine hupenda kula chukuchuku (kuweka chumvi bila kuchanganya na kitu kingine). “Raha ya panya unakula kila kitu hadi mifupa, ni wanyama shambani lakini nyumbani ni mboga. Mara nyingi tunapenda kula baada ya kumchoma halafu ndio unaiunga,” anasema Mkuti. Samwel Minjale Mkazi wa Kijiji Chikoweti, anasema katika maisha yake amejifunza kula vyakula vingi lakini amevutiwa zaidi kula panya kitoweo ambacho ni rahisi kupatikana. “Mimi namfahamu kwa kumla na si kwa kumsikia, huwezi kumfananisha na samaki kwani ana mafuta ya pekee na hutumii nguvu kumuandaa. “Huwezi kumfananisha na kiumbe mwingine wala kuku, yaani panya ukishamkamata unamchoma na ana mafuta ya kujitegemea ila unaongeza chumvi tu,” anasema Minjale.   MITEGO Mzee Mpupua ambaye anajishughulisha kutengeneza mitego ya panya,  anasema kazi hiyo ameifanya kwa zaidi ya miaka 36. “Nilianza kutengeneza mitego mwaka 1982 na maisha yangu kwa kiasi kikubwa naendesha kwa biashara hii,” anasema. Anasema uuzaji wa panya umeshamiri katika miaka ya hivi karibuni baada ya wategaji kuongezeka hali iliyosababisha kupandisha bei ya mitego. “Awali nilikuwa nauza mtego kwa Sh 100 baadae ikapanda hadi Sh 200, hivi sasa nauza mitatu kwa Sh 1,000 na tunaofanya biashara hii siku hizi ni wengi. “Mara nyingi huwa tunakwenda porini tunawavuna panya kisha tunawakausha kwa moto na kuwauza kwa mafungu. Nimekuwa nikimaliza mipango midogo midogo ya kifamilia kwa kuuza panya na mambo yamekuwa yakienda sawa,” anasema Mpupua.   SOKO LA PANYA Soko kubwa la panya liko katika maeneo ya Mtandi, Migongo, Mwimbaka, Mbarika na Kanyimbi ambako ndiko kuna wateja wengi wa kitoweo hicho. Kitoweo hicho huuzwa kwa mafungu ya panya watano kwa Sh 500 na fungu lingine ambalo huwa na panya wanane ambao ni wakubwa huuzwa Sh 1,000. Anasema kwa siku wanaweza kuvuna zaidi ya panya 2,000. Hata hivyo, Mpupua anasema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika utegeji wa kitoweo hicho na hivyo wakati mwingine kuhatarisha maisha yao. “Tunapata shida kwa sababu wengi wetu tunatembea bila kuvaa viatu, hata wanaovaa wamekuwa wakitumia viatu ambavyo haviwazuii kujikinga na wanyama hatari kama nyoka na wengineo,” anasema Mpupua.   MTAALAMU WA LISHE Ofisa Lishe Mkoa wa Mtwara, Herieth Kipuyo, anasema ulaji wa nyama una faida kubwa kwenye mwili wa binadamu. “Unajua panya yupo kwenye kundi la vyakula vyenye protini, yupo katika kundi la nyama kati ya makundi matano ya vyakula. Makundi haya yana umuhimu ndani ya mwili wa binadamu kwa kuujenga ili uweze kufanya kazi vizuri. “Lakini siwezi kusema moja kwa moja kwamba nyama ya panya ni muhimu kwa kiasi gani au ina madhara kiasi gani,” anasema Kipuyo.
0
RAMADHAN HASSAN-DODOMA KATIBU wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humprey Polepole, amesema idadi kubwa ya mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) yamepoteza mwelekeo wa kuwahudumia wananchi, hivyo nafasi hiyo inapaswa kuchukuliwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kusemea na kutatua kero za wananchi. Kauli hiyo aliitoa mwishoni mwa wiki jijini hapa wakati akifungua mafunzo ya siasa na uenezi kwa makatibu uenezi wa CCM Wilaya ya Dodoma. “Mimi nilishawahi kuwa kiongozi mkubwa kwenye NGO’s lakini kwa sasa asilimia kubwa ya NGO’s zinapoteza mweleko. Nafasi hiyo inapaswa kuchukuliwa na wana-CCM,” alisema. Alisema viongozi wa CCM wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa kuzingatia maadili na matendo mema katika kuwatumikia wananchi. Alisema chama kitaendelea kuwatumikia wananchi na hakitakubali kuyumbishwa na  wapinzani katika kutatua kero za wananchi. Aidha, aliwataka makatibu uenezi kutotumia lugha za matusi dhidi ya wapinzani, bali wanapaswa kutumia nguvu ya hoja. “Kiongozi wa CCM kutumia lugha ya matusi ni kwenda kinyume na maadili ya chama. Msiwaite wanachama wa vyama vingine nyumbu,” alisema. Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma, Godwin Mkanwa, alisema katika uchaguzi mkuu uliopita, walipoteza kata sita ambapo tayari kata nne zimerejea CCM, bado kata mbili ambazo wana uhakika katika uchaguzi mkuu ujao watashinda kwenye kata zote.
3
SERIKALI imezungumzia kupanda kwa bei ya vyakula nchini hususani nafaka. Imesema hali hiyo imetokana na serikali kuondoa ukiritimba, kwa kuruhusu ushindani katika uuzaji mazao ya kilimo.Hata hivyo, imetoa matumaini kwamba pamoja na ongezeko la mahitaji hususani ya mahindi ndani na nje ya nchi kuchangia bei kupanda, miezi michache ijayo itashuka, kwani wakulima wataanza kuvuna mashambani. Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alisema hayo hivi karibuni katika mahojiano maalumu na gazeti hili juu ya hali halisi ya kupanda kwa mahindi, unga, mchele, maharage katika maeneo mbalimbali nchini. “Awali tulizuia mazao yasiuzwe nje ya nchi. Tunapofungua mipaka kuuza nje ya nchi, ushindani umechukua nafasi ndiyo sababu ya bei kupanda. Lakini ikifika Februari bei itashuka, mazao yataanza kutoka mashambani,”alisema Bashe.Alisema mahitaji ya mahindi, yamekuwa makubwa siyo tu nchini, bali pia kwa nchi zinazozunguka Tanzania.“Ni fursa kwa wakulima. Naendelea kuhamasisha wakulima zalisheni kwa kiwango chochote mnachoweza, hakuna wa kuingilia soko lenu, wapi na bei gani muuze” alisema.Akisisitiza msimamo wa serikali wa kutoingilia bei ya mazao ya wakulima, Bashe alisema bei inayoonekana sasa, ndiyo thamani halisi ya mkulima. “Hatutaingilia kupunguza bei ya mazao. Wakati unajiuliza swali la bei kupanda, jiulize mwaka jana mkulima alikuwa ananunua saruji au bati kwa bei gani?“Tulijenga utamaduni wa kuingilia na kumdhibiti mkulima. Akilima ni zao lake binafsi, lakini akivuna linageuka kuwa mali ya umma. Bei imepanda kwa sababu tumeruhusu soko lichukue nafasi yake na bei inatokana na demand and supply,” alisema.SOKO NCHI ZA NJEKwa mujibu wa Bashe, mahitaji ya mazao yamekuwa makubwa ndani na nje ya nchi. Miongoni mwa nchi ambazo zimeanza kununua mahindi nchini ni Zimbabwe kupitia Wakala wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na Burundi na Rwanda kupitia Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB). Pia wafanyabiashara binafsi, wameachiwa uhuru wa kuuza nje ya nchi.Akizungumzia mahitaji ya mahindi, naibu waziri huyo alisema wigo umepanuka, kwani awali yalichukuliwa kama ni zao la chakula cha binadamu tu, lakini sasa yanatumika pia kama chakula cha wanyama na kuku.Akieleza serikali inavyohakikisha wakulima wananufaika na si wafanyabiashara pekee, Bashe alisema inawapa taarifa sahihi, kwa kuwaambia bei halisi ya mazao kwenye masoko, kama vile jijini Dar es Salaam kisha wao wanaamua.NFRA na CPB ambazo ni taasisi za serikali, pia zinapokwenda kununua mazao kwa wakulima, zinatoa bei shindani, ambayo inafanya pia wafanyabiashara kutoa bei iliyo nzuri zaidi. Bei ilivyopaa Jijini Dar es Salaam, kiroba cha unga wa sembe cha kilogramu tano, ambacho takribani miezi mitatu iliyopita kilikuwa kikiuzwa kati ya Sh 5,000 na 6,000, sasa kinauzwa Sh 8,000.Mchele ambao kilogramu iliuzwa kati ya Sh 1,500 na 2,000 kulingana na kiwango chake, sasa unauzwa kati ya Sh 1,700 na 2,200. Katika maeneo yanayozalisha mazao ya chakula kwa wingi mfano Rukwa, gazeti hili limebaini mjini Sumbawanga na mji wa Namanyere wilayani Nkasi, bei ya na mahindi imepanda maradufu.Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili, mfanyabiashara wa nafaka anayemiliki ghala la nafaka (Mwanafyale Store) mjini Sumbawanga, Bukuku Mwanafyale alisema gunia la mahindi lenye kilogramu 100 ambalo lilikuwa likiuzwa Sh 18,000, sasa linauzwa kati ya Sh 96,000.Mjini Namanyere bei ya mahindi imepanda kutoka Sh 30,000 kwa gunia lenye kilogramu 100 hadi Sh 84,000. Bei ya mchele imepaa kutoka Sh 1,500 kwa kilogramu hadi Sh 2,000.“Debe la mahindi lenye ujazo wa lita 20 lilikuwa likiuzwa shilingi 5,000 miezi michache iliyopita lakini sasa linauzwa shilingi 14,000,” alisema mkazi wa Nkasi, John Nusurupia. Mjini Sumbawanga bei ya rejareja ya mchele, imeporomoka kutoka Sh 2,300 hadi kati ya Sh 1,500 na 1,700 kwa kilo kulingana na ubora wake. “Mara nyingi kila msimu bei ya mahindi ikipanda basi bei ya mchele inaporomoka,”alisema mchuuzi wa mchele, Semeni Ally.Kutoka Mkoani Tanga, gazeti hili limebaini kuwa licha ya wakulima wa mahindi wa wilaya za Muheza, Mkinga, Handeni, Korogwe na Kilindi kuvuna mahindi, baadhi ya wafanyabiashara wa mahindi bado wanauza bei kubwa, ambapo gunia moja lenye uzito wa kilogramu 100 linauzwa kati ya Sh 70,000 hadi Sh 80,000.Mfanyabiashara wa mahindi katika soko la mahindi la Ngamiani na Barabara 15 jijini Tanga, Juma Ally alisema “Kwa sasa hali ya mazao kama mahindi yamepanda bei sana ambapo gunia moja la mahindi tunauziwa na wakulima kwa kati ya shilingi 65,000 na 70,000, tunapoyasafirisha hadi kwenye soko na sisi ili tupate faida tunauza kati ya shilingi 70,000 hadi 80,000 kwani bila kufanya hivyo hatuwezi kupata faida”.Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wakulima wa mahindi kutoka wilaya za Muheza, Kilindi,Korogwe na Mkinga walimpongeza Rais Dk John Magufuli, kwa kutambua mchango na juhudi kubwa zinazofanywa na wakulima, kwani kwa muda mrefu wakulima walikuwa wakilanguliwa na wafanyabiashara wakubwa.Kenedy Massawe, mkulima wa mahindi Wilaya ya Korogwe alisema baadhi ya wakulima wa mahindi, walikuwa hawanufaiki na zao hilo kutokana na wafanyabiashara kutoka Kenya kuja kwa wakulima na ‘kuchumbia’ mahindi yangali shambani, hivyo mkulima alikuwa hanufaiki na kilimo hicho.Ufafanuzi wa Naibu Waziri, Bashe, kuhusu kupanda kwa bei ya vyakula, hautofautiani na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga aliowahi kutoa mwaka jana, akisema hakuna uhaba wa chakula isipokuwa mahitaji ya soko, ndiyo yameongezeka na kusababisha bei kupanda.Habari hii imeandikwa na Stella Nyemenohi, Dar, Cheji Bakari, Tanga na Pety Siyame, Sumbawanga.
3
TAASISI ya Mashauriano ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika (AALCO), imetakiwa kusimama kidete katika kulinda maslahi ya nchi zinazoendelea, kwa kuweka utaratibu mzuri na sheria za kimataifa dhidi ya mataifa yanayochochea migogoro katika nchi hizo, kwa maslahi yao binafsi.Pia, taasisi hiyo imeombwa kuonesha mchango wake na kupaza sauti katika jitihada za kuyashawishi mataifa yaliyoiwekea vikwazo vya kiuchumi nchi ya Zimbabwe, kuondoa vikwazo hivyo.Hayo yalibainishwa jijini Dar es Salaam jana na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan wakati akifungua Mkutano wa 58 wa AALCO uliokutanisha washiriki zaidi ya 150 kutoka mataifa mbalimbali wanachama wa taasisi hiyo.“Leo hii tunashuhudia vita ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi mbalimbali zinazoendelea zilizosababishwa na mataifa yenye ubinafsi kwa lengo la kujichukulia rasilimali katika nchi hizo zenye migogoro,” alieleza Samia.Alisema ni wakati wa taasisi hiyo kusimama kidete na kuweka taratibu nzuri na sheria za kimataifa zitakazodhibiti mataifa hayo yenye ubinafsi. Pamoja na hayo, aliiomba taasisi hiyo kupitia mkutano huo kusaidia kuhamasisha mataifa yaliyowekea vikwazo nchi ya Zimbabwe kuviondoa kwa kuwa kwa sasa nchi hiyo ni taifa huru linalojitegemea.“Serikali ya Tanzania tunaamini kuwa wanachama wa AALCO kupitia mkutano huu watatumia sauti zao kuhakikisha wanaendeleza kanuni ya kutoingilia mambo ya ndani na heshima kwa uhuru wa dola husika,” alieleza.
3
RAIS John Magufuli amesema serikali imefanya kila liwezekano, kuboresha jiji la Dodoma ili liwe la mfano na kutimiza ndoto za Baba wa Taifa, hayati Julius Nyerere za mwaka 1972 kuwa za ukweli.Aliwataka pia wakazi wa Dodoma, kufanya kazi na wasichague kazi ili mradi inawapa riziki. Aliwataka watumie fursa ya kunyesha mvua, kuzalisha mazao mengi. Akizungumza katika mkutano wa hadhara, uliofanyika Soko la Kimataifa lililopo Njuguni jijini hapa jana, alisema juhudi hizo za serikali zimeenda pamoja na kupandisha hadhi ya mji kuwa jiji.Alisema serikali imeamua kuboresha kwa kuanzisha miradi mbalimbali, kama ya stendi itakayounganisha na kituo cha Reli ya Kisasa (SGR) na Mji wa Serikali kwa treni maalumu na pia itaunganisha na Uwanja wa Ndege wa Msalato kwa barabara.Rais Magufuli alisema serikali pia imetoa Sh bilioni 415 kwa ajili ya kujenga barabara ya njia nne ya mzunguko zenye urefu wa kilometa 110 kuanzia Nala, Veyula, Mtumba hadi Ihumwa, kwa lengo la kupunguza msongamano katikati ya jiji na kupitisha magari nje ya mji. Magufuli alisema pia serikali imetoa fedha kwa ajili ya kujenga Uwanja wa Ndege wa Msalato, ambao utagharimu Sh bilioni 500 na utakuwa na uwezo wa kutua ndege zote kubwa duniani.Kuhusu fursa Rais Magufuli aliwataka wananchi wa Dodoma, wajipange wazitumie fursa za uwepo wa makao makuu ya serilai na miradi mbalimbali inayotekelezwa jijini humo.“Fursa zipo, ukiuza nyanya una uhakika wa soko, tikiti maji soko lipo, ng’ombe na kuku soko lipo, mtama au uwele, vitunguu soko lipo, litumieni soko na fursa hiyo, mkichelewa wengine watazikamata nanyi mtabaki kuwa watazamaji… nawaomba watu wa Dodoma tuitumie fursa kwa ajili ya kujenga uchumi wetu, kuwa na mitazamo ya maendeleo, serikali imetimiza wajibu wake na uchumi wa mtu mmoja ni jukumu lenu,” alisema.Kuhusu kuhamia Dodoma Rais Magufuli alisema serikali imeboresha jiji la Dodoma ili liendane na hadhi ya makao makuu ya nchi na imefanya kwa vitendo.“Wapo wengine hawakuamini, walisema ni maneno tu, walikebehi, lakini leo mwenye macho haambiwi tazama. Dodoma ndio jiji la kupendeza,” alisema.Alisema kuhamia huko ni kutekeleza ndoto ya Mwalimu Julius Nyerere ya tangu 1972, ambayo amekuja kutimiza sasa zaidi ya miaka 42. Rais Magufuli alisema wakati anapandisha hadhi ya Dodoma kuwa jiji Aprili 26 mwaka jana, aliahidi kwamba ifikapo 2020 serikali ingekuwa imehamia Dodoma, lakini leo serikali yote imehamia Dodoma.“Wizara zote zipo hapa, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu walikwishahamia na mimi pia nimekwishahamia tangu Oktoba 2019, tunawashukuru kwa kutupokea vizuri,” alisema.Kuhusu miradi ya soko, stendi Rais Mafuguli alisema soko hilo litaitwa Ndugai, ambaye ni Spika wa Wabunge, kutokana na wakati Bunge linapitisha azimio na sheria ya Dodoma kuwa makao makuu alikuwa Spika.Alisema Ndugai angeweza kupinga, lakini hakupinga, lakini pia anafanana naye. “Ndugai nafanana naye kidogo, Soko likiitwa Ndugai ... ni vema kumkumbuka. Soko hilo si la wana Dodoma pekee, bali ni la kimataifa. Tumkumbuke Spika kwa kulipa soko hilo jina hilo la kimataifa,” alisema.Alimtaka mkandarasi kukamilisha soko na stendi kwa wakati hadi Februari 15, mwakani, kama alivyoahidi. Alisisitiza kuwa hakuna muda wa nyongeza. Alimpongeza Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda kwa kuamua kuwekeza Dodoma na aliwataka wakazi wa Dodoma, kujifunza kwake ili yeye awe mwalimu, nao wawe wanafunzi.Aliwapongeza viongozi wote kwa Dodoma, kwa kufanikisha miradi hiyo, kwa kufanya mabadiliko ya jiji, hasa mtindo wa kuweka rangi kwenye mabati ambayo ni mtindo wa pekee nchini.“Mkurugenzi wa Jiji sikukuamini, sasa nawaamini vijana kwamba wanaweza kufanya kazi vizuri” alisema.Changamoto za ardhi Rais Mafuguli alisema katika orodha ya kero za ardhi alizompa Mkuu wa Mkoa, zipo za ukweli na zipo za uongo. Alisema wapo watu wanafiriki kwamba ujio wa serikali ni fursa ya kutengeneza fedha. Alisema Sheria ya Ardhi Namba 4 na 5 za mwaka 1999, inasema ardhi ikichukuliwa lazima alipwe fidia, kwa hiyo aliyekaa katika eneo kwa kuvamia, anatakiwa kuilipa serikali.Rais Magufuli alisema wanapopekeka madai mbele ya serikali, lazima wapime, kwani wamejitokeza matapeli na wanajifanya wenyeviti wa kudai ardhi, wanawalia fedha wananchi. Alisema wananchi kujiepusha na matapeli wa kukusanya fedha na mawakili wa ajabu ajabu. Alisema serikali ina mbinu za kufanya kazi na utapeli ni kosa la jinai.“Niliwaleta viongozi makini, mkuu wa mkoa alitoka Ruvuma, wakurugenzi, ma-DC, RAS na watendaji, wabunge na madiwani, mkishikamana mtapata suluhisho.“Serikali haina fedha za kutoa bure. Wanaodai fidia watakuwa wanakwamisha maendeleo, kwani haikuwa lazima kuleta makao makuu, yangeweza kupelekwa Singida Sukamahela ambapo ni kati kati, lakini Nyerere alipapenda hapa, msimfanye Baba wa Taifa apate machungu,” alisema.Katika hatua nyingine, Spika wa Bunge, Job Ndugai ameshukuru rais John Magufuli kwa kumpa heshima kubwa ya kutaka soko la kisasa liitwe kwa jina Soko la Ndugai. Ndugai alisema hayo jana jijini hapa, wakati wa kufunga Mkutano wa Sita wa Bunge la Vijana 2019, lililokutanisha wanafunzi 58 kutoka vyuo 30 hapa nchini.“Muda mfupi kabla sijafika hapa, Rais John Magufuli ameagiza soko la kisasa analoliwekea jiwe la msingi liitwe Soko la Ndugai, jambo hili limenipa heshima sana, namshukuru sana Rais… nikiwa nimesimama katikati ya watani zangu Wasukuma, wamekuwa wakiniambia simama! Simama! Ila sasa nimeonekana kumbe na mimi ni mrefu, kwa niaba yangu, familia yangu na wananchi wangu wa Kongwa, namshukuru sana Rais kwa heshima hii ya kipekee aliyonipa,” alisema Ndugai.
4
Hatua hiyo ya kutenga ekari 160 katika eneo la Jitegemee, upande wa barabara ya Mandela inayolenga kuongeza ufanisi wa bandari hiyo kubwa hapa nchini na kuifanya kuwa shindani.Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe alitangaza hatua hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam katika mkutano wa kuhitimisha ziara ya ujumbe wa maofisa wa serikali na wafanyabiashara kutoka jimbo la Katanga, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.Ujumbe huo uliokuwa na lengo la kuimarisha biashara kati ya nchi hizo uliongozwa na Naibu Gavana wa jimbo hilo, Guibert Tshibal na waziri wa Uchukuzi wa jimbo hilo, Laurent Kahozi Sumba.Waziri Mwakyembe aliwaambia waandishi wa habari kuwa sehemu ya ardhi hiyo itawekwa kwa ajili ya jumuiya ya wafanyabiashara wa Kongo DRC.“Tunafanya hivi kwa nia ya kuimarisha bandari yetu na pia biashara na majirani zetu,” alisema.Mizigo ya DRC imekuwa ikiongezeka kwa asilimia takribani 24 kwa mwaka tangu mwaka 2004 ikiongezeka kutoka tani 155,611 hadi tani 1,117,249 mwaka 2013. Nchi ya DRC ni ya pili kwa kupitisha mizigo mingi katika bandari ya Dar es Salaam.Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, mizigo ya DRC inachukua asilimia 25 ya mizigo yote ya nchi jirani inayopita katika bandari hiyo. Pamoja na mambo mengine, ujumbe huo ukiwa nchini ulitembelea eneo hilo pamoja na bandari ya Dar es Salaam.Waziri Mwakyembe alisema kuwa kamati ya ufundi iliyoundwa na wajumbe wa nchi hizo imekubaliana kushughulikia kero zote zinazokwamisha biashara kati ya nchi hizo. Kwa upande wake, Kahozi Sumba alisifu juhudi za Tanzania kwa hatua inazochukua kuimarisha bandari ya Dar es Salaam.“Tutazidi maradufu kutumia bandari hii,” alisema. Alisema kuwa bandari hiyo ni njia kuu ya kupitishia mizigo kwa nchi yake hivyo kuimarishwa kwake kutaleta nafuu ya maisha katika jimbo hilo na nchi ya DRC kwa ujumla.Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande alisema kamati hiyo ya ufundi imekubaliana pia kuwa na orodha ya kampuni za wakala wa kupakia na kupakua mizigo katika nchi zote ili kuepuka wizi na matatizo mengine.Pia ilikubaliwa ianzishwe bandari kavu katika eneo la mpaka wa DRC na Zambia la Kasumbalesa ili kupunguza na kuondokana na tatizo sugu la msongamano wa malori ya mizigo. Kwa upande wake, Tshibal alisifu juhudi zinazofanywa na Dk Mwakyembe na serikali nzima za kuimarisha sekta ya usafiri.“Dk Mwakyembe ni hazina kwa Tanzania...ni mtu wa vitendo,” alisema Naibu Gavana huyo. Ziara hiyo imekuja kufuatia ile iliyofanywa na wenzao wa Tanzania katika jimbo hilo mapema mwezi Mei mwaka huu ambapo TPA ilifungua ofisi yake ndogo ya mawasiliano katika mji wa Lubumbashi.
5
WASHINGTON, MAREKANI HATUA ya kuongezeka kwa uhifadhi na usimamizi wa maeneo ya pekee ya Kusini mwa Tanzania na kukuza viumbe mbadala kwa jamii   vijijini na maendeleo ya miundombinu, kunatajwa kama sababu za kuwa sehemu salama kwa utalii nchini. Pia inaelezwa kwamba hali hiyo itachangia kuweapo   fursa za  uchumi kwa kanda, kulinda mali ya asili  ambako kaya zaidi ya 40,000 zinaweza kufaidika na fursa hizo. Hayo yalisemwa   jijini Washngton, Marekani na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa   Tanzania, Malawi, Somalia na Burundi, Bella Bird. Alikuwa  akitangaza matokeo ya utafiti kwa kipindi cha miaka sita ijayo kupitia mkopo wa Dola milioni 150 zilizotolewa na Chama cha Kimataifa cha Maendeleo kwa njia ya Usimamizi wa Rasilimali za Utalii na mradi wa Kukuza Uchumi (Regrow),  uliopitishwa Septemba 28, mwaka huu na Benki ya Dunia. “Lengo la Regrow ni kuboresha usimamizi wa rasilimali za asili na mali za utalii katika maeneo ya kipaumbele ya Kusini mwa Tanzania na kuongezeka shughuli za uendeshaji mbadala kwa jumuiya husika,” alisema Bird. Alisema  pia kuwa itasaidia kukuza uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa na mbuga za wanyama, kupunguza mgogoro kati ya binadamu na wanyamapori na kuimarisha ustahimilivu wa mazingira magumu na mabadiliko na kuchangia kwenye mtiririko wa ulinzi kutoka Mto Ruaha kwenda kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ruaha. “Utalii ni kipengele muhimu cha uchumi wa Tanzania na ulichangia kwa asilimia 10 ya Pato la Taifa mwaka 2015. “Nchi hii imepewa viumbe hai na vivutio vya wanyamapori, lakini watu wengi wanafahamu zaidi vivutio vilivyopo Kaskazini mwa Tanzania. “Vivutio vilivyopo Kusini vinaweza kuongeza idadi ya watalii   nchini na hivyo kuongeza faida za  uchumi na kukuza uhifadhi wa wanyamapori. Ili iwe hivyo, miundombinu na huduma zinahitajika kuboreshwa,” alisema Bird. Alivitaja vivutio vilivyopo Kusini mwa Tanzania kuwa ni Hifadhi za Katavi, Kitulo, Mahale, Milima ya Udzungwa, Mikumi na Ruaha na vivutio vinginevyo kama mbuga ya Selous, maziwa ya Nyasa na Tanganyika na vinginevyo.
3
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya,  alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele.  “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema
5
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019  kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na  kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi  kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na  kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza.  “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake.
5
LIGI Kuu ya soka ya wanawake msimu wa 2019/20 inatarajiwa kuanza leo ambapo Simba Queens na Yanga Princess zitakuwa kwenye viwanja tofauti kuanza kampeni zake. Timu 12 zinashiriki ligi hiyo ambayo taji lake linashikiliwa na JKT Queens.Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Simba itakuwa mwenyeji wa Ruvuma Queens kwenye uwanja wa Karume Dar es Salaam huku mahasimu wao, Yanga wakiwa ugenini kukabiliana na Tanzanite Queens kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.Michezo mingine bingwa mtetezi wa ligi JKT Queens itakuwa ugenini kucheza na Baobab Queens kwenye uwanja wa Jamhuri Dodoma. Alliance Girls watawakaribisha Kigoma Sisterz kwenye Uwanja wa Nyamagana Mwanza, wakati Mlandizi Queens watawakabili Panama Girls kwenye Uwanja wa Mabatini Pwani huku TSC Queens watakuwa kwenye Uwanja wa Gwambina kucheza na Marsh Queens.Akizungumza jana mwenyekiti wa kamati ya soka ya wanawake, Amina Karuma alisema ligi hiyo imezidi kupata nguvu kila wapofungua msimu. Alisema ligi hiyo itachezwa raundi mbili kisha itasimama kupisha maandalizi ya kikosi cha timu ya Soka ya taifa ya wanawake ya Bara, Kilimanjaro Queens kujiandaa na michuano ya Chalenji inayotarajiwa kuanza mwezi ujao nchini.“Ligi inaanza na kikubwa bado tunasisitiza kuomba sapoti kutoka kwa wadau wa mchezo wa soka kutuunga mkono kama mpira wa kiume ili teendelee kupata wadau wengi zaidi watakaokuwa tayari kutoa pesa kudhamini ligi yetu kisha kutoa fursa kwa timu zingine kushiriki,” alisema Amina.
4
TIMU ya taifa ya waendesha baiskeli ya Rwanda iko katika maandalizi makali kwa ajili ya mashindano ya Afrika yaliyopangwa kufanyika katika mji wa Bahir Dar, Ethiopia, imeelezwa.Hayo ni mashindano ya 14 ya kila mwaka tangu kuanzishwa kwake mwaka 2005. Wapanda baiskeli bora Afrika wiki hii watakuwa njiani kuelekea katika mashindano hayo makubwa yatakayoshirikisha timu za taifa.Rwanda ilikuwa mwenyeji wa mashindano kama hayo mwaka jana. Akizungumza na waandishi wa habari juzi, kocha wa timu ya vijana ya (wanaume na wanawake) na ile ya wanawake ya wakubwa, Nathan Byukusenge alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na wanaangalia mbele kwa wapanda baiskeli wao kufanya vizuri Ethiopia.“Maandalizi yetu yanaendelea vizuri, na wachezaji wetu wako vizuri tayari kwa mashindano hayo ya Addis Ababa, tuko tayari kukabiliana na wapanda baiskeli bora Afrika, tunajiamini na uwezo wetu,” alisema Byukusenge, ambaye aliwakilisha nchi katika mashindano ya Mountain Bike katika Olimpiki ya 2016 Rio, Brazil.
4
Na JANETH MUSHI, ARUSHA MAHAKAMA Kuu Kanda ya Arusha, leo inatarajia kusikiliza rufaa ya maombi ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), anayeshikiliwa katika mahabusu ya Gereza Kuu la Kisongo, jijini hapa. Kusikilizwa kwa rufaa hiyo kunatokana na uamuzi wa mahakama hiyo uliotolewa Desemba 20, mwaka huu na Jaji Dk. Modesta Opiyo, ambaye alikubali maombi namba 69 ya Lema ya kuomba kuongezewa muda wa kuwasilisha notisi ya nia ya kukata rufaa ya dhamana yake. Wakati akikubali maombi hayo, Jaji Dk. Opiyo alitoa siku 10 kwa ajili ya mleta maombi ambaye ni Lema, kuwasilisha notisi hiyo. Rufaa hiyo namba 126 ya mwaka huu, iliyokatwa na mawakili wa Lema, wakiongozwa na Sheck Mfinanga, inatarajiwa kusikilizwa na Jaji Salma Maghimbi wa mahakama hiyo, leo saa tatu asubuhi. Akizungumza na MTANZANIA kwa simu jana, Wakili Mfinanga alisema kuwa, lengo la rufaa hiyo ni kupinga na kudai haki ya dhamana ya Lema aliyonyimwa kutokana na makosa ya kisheria yaliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Novemba 8, mwaka huu. Wakili Mfinanga alisema kuwa, wameamua kukata rufaa hiyo ili kujua ni kwanini Lema amekosa dhamana ambayo awali katika mahakama hiyo, alipewa na kuwa hawaridhiki na uamuzi uliotolewa na Hakimu Desderi Kamugisha, aliyemnyima dhamana. Alisema kwamba, Hakimu Kamugisha alisema mahakama hiyo inampa Lema dhamana kwa masharti itakayoyaweka, lakini kabla hajamalizia kutoa uamuzi wake, mawakili wa Serikali walisema wameandaa notisi ya rufaa juu ya uamuzi huo na hoja hiyo ikakubaliwa na hakimu huyo. Lema alikamatwa Novemba 2, mwaka huu, nje ya Bunge mjini Dodoma na tangu wakati huo, yuko mahabusu akituhumiwa kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli kupitia mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali jijini hapa.
3
Na RAMADHAN HASSAN -DODOMA KATIBU Mkuu wa Chama  Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amesema kwa sasa viongozi madalali  wanaouza viongozi ndani ya chama hicho hawatakiwi, huku akiwataka watafute kazi nyingine za kufanya. Kutokana na hali hiyo amesema sasa wamejipanga kuhakikisha CCM inaendelea kutawala maisha yote huku akiwataka wenyeviti wa kata, wilaya na mikoa kutokuwa na sehemu ya malalamiko na badala yake wawe sehemu ya kusimamia Serikali kama anavyofanya Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Dk.  John Magufuli. Kauli hiyo aliitoa jana mjini hapa katika kilele cha maadhimisho ya miaka 40 ya CCM yaliyofanyika katika ukumbi wa Dodoma Convention Centre, ambao unamilikiwa na chama hicho, ambapo Kinana awalitaka viongozi wa chama hicho kuacha kuwa walalamikaji na badala yake wawe sehemu ya kuisimamia Serikali katika kutimiza wajibu wake. “Sasa hatutaki kuwa na viongozi madalali ndani ya chama, kwa hiyo kama wapo wajitafakari wenyewe. Ndiyo maana hata sisi tumekubaliana maadhimisho sio sherehe lazima tuachane na tabia za sherehe ukisema sherehe itabidi pia mlipane na posho jambo ambalo halikubaliki,’’ alisema Kinana. Akielezea sababu za kuendelea kushinda kwa chama hicho katika chaguzi mbalimbali, Kinana alisema wamekuwa wakisimamia na kupigania haki za wananchi huku akidai kwa sasa kuna viongozi wamekuwa madalali ndani ya chama hicho. “CCM ni chama chenye nguvu wana CCM wamekuwa wamoja na hiyo ndiyo imetufanya tumekuwa tukiendelea kuaminiwa na wananchi na sababu zipo wazi ni kusimamia na kupigania haki zao hakuna mwenye kauli wana CCM wanamuunganiko. “Sababu nyingine ya kuendelea kuaminiwa ni uwepo wa demokrasia pana na yenye kina kwa kila mwanachama kuwa na uhuru wa mawazo kwa kusema na hata kushauri. “Wanaoamua ndani ya chama ni wanachama wakisema ndiyo ni ndiyo na wakisema hapana ni hapana katika uchaguzi mwanachama ana haki ya kuchagua na ana uhuru wa kuchukua fomu na kugombea,’’ alisema Kinana. Alisema kwa sasa vipo vyama vitatu pekee duniani ambavyo vinaoongoza kwa maandiko mazuri na yenye tija  ambapo alivitaja vyama hivyo kuwa ni Chama cha Kikomunisti cha China, CCM na ANC cha Afrika Kusini. Kinana  alisema mwaka 2015 chama hicho kilifanya tathmini kwa miezi 12 kuanzia katika shina mpaka taifa lengo likiwa ni kupunguza urasimu na umangimeza, ambayo iliwasaidia kujua upungufu na marekebisho wanayotakiwa kufanywa. Kuhusu suala la Serikali kuhamia Dodoma, alisema Serikali inatakiwa iungwe mkono japo alikiri kwamba mwanzo utakuwa mgumu. Pia aliwataka wanachama wa chama hicho kuchagua viongozi wenye kazi zao katika uchaguzi mbalimbali utakaofanyika. “Muwachague viongozi bora waadilifu wenye shughuli zao zisizotokana na CCM awe na shughuli ya kufanya,’ ’alisema. Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, alisema CCM kimehusika kwa asilimia kubwa katika kuleta amani na utulivu nchini huku akiponda vyama vingine kuhusika na maandamano kila kukicha. “Hivi vingine ni vyama vya maandamano tu, amani na utulivu imeletwa na CCM kumbukeni zamani tulikuwa tunasema chuo kikuu sasa hivi tunasema vyuo vikuu  Udom pekee wanamaliza wanafunzi 36,000,’’ alisema Mangula. Maadhimisho ya miaka 40 kwa mwaka huu yamekuwa ya aina yake ambapo yamehudhuriwa na wabunge wote wa chama hicho, wakiwamo mawaziri wakuu wastaafu, John Malecela na Mizengo Pinda pamoja na Spika wa Bunge, Job Ndugai.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amehimiza mashabiki wa soka nchini kuiunga mkono timu ya taifa kuelekea katika michezo ya kufuzu Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) na Kombe la Dunia kwa kuhakikisha wanajaza uwanja.Majaliwa ameyasema hayo Dar es Salaam kwenye tamasha la kilele cha wiki ya Simba, ambapo aliwaeleza mashabiki wa klabu hiyo kama walivyojaza uwanja wafanye pia, kwa timu ya taifa.“Tunatambua mwezi ujao timu ya taifa zitacheza hapa dhidi ya Burundi na Sudan, tujitokeze kama ambavyo mmejitokeza wanasimba kwa kujaza uwanja,”alisema.Alisema ni wakati sasa kuendelea kuonesha mshikamano wa dhati kwenye maendeleo ya michezo.Waziri Mkuu alisema, “tunaridhishwa sana na maendeleo ya soka Tanzania. Soka letu limeanza kukua kwa kiwango kizuri. Tumeona timu zetu za taifa zinashinda kila siku. Juzi tumewashinda Kenya, na tena timu ya akina mama iliwafunga Eswatini,”Alisema mafanikio yanayoonekana kwa timu ya taifa ni matokeo ya kuwa na klabu imara ikiwemo Simba, Yanga, Azam, KMC na Namungo.Timu ya taifa baada ya kuitoa Kenya hivi karibuni katika mchezo wa marudiano inatarajiwa kucheza na Sudan katika raundi ya mwisho ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Chan nchini Cameroon 2020.Taifa Stars imepangiwa kuanza na Burundi katika mechi ya awali ya kufuzu kwa Kombe la Dunia, ambalo fainali zake zitafanyika Qatar 2022.
4
Simba juzi ilitumia dakika 120, kupata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho msimu ujao, baada ya kuifunga Mbao FC mabao 2-1, katika mchezo wa fainali ya michuano ya FA kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma.Akizungumza na gazeti hili Omog, alisema wachezaji wake walicheza kwa juhudi kubwa muda wote wa mchezo ndiyo maana wakapata ushindi huo na kutimiza malengo yao kwa kutwaa taji hilo. “Nawapongeza sana wachezaji wangu walicheza kwa nidhamu na kujituma muda wote wa mchezo, na hiyo inatokana na mikakati tuliyokuwa tumejiwekea ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kukosa taji la Ligi Kuu Bara,” alisema Omog.Kocha huyo raia wa Cameroon pia hakusita kuwapongeza wapinzani wao Mbao FC, kwa kuonesha ushindani wa kweli na kusema walistahili kucheza fainali. Kwa upande wake kocha wa Mbao, Mrundi, Etienne Ndayariagije alizungumzia masikitiko yake dhidi ya mwamuzi aliyechezesha mpambano huo kuwa hakuwatendea haki, baada ya kuwapa Simba penalti isiyokuwa halali.Ndyariagije alisema kwa sheria za Shirikisho la Soka wanakubali kuwa wamefungwa, lakini wao binafsi wanajua kuwa ndiyo mabingwa wa taji hilo, kwani walistaili kutokana na kiwago bora walichokionesha na kuwabana miamba hiyo ya soka nchini “Mwamuzi alijitahidi sana,lakini mwishoni alibadilika na kutoa maamuzi ambayo ni wazi yalionesha kuibeba Simba, hiyo haipendezi kwa sababu lengo siyo ubingwa lakini pia uwezo wa timu ili huko inapokwenda ikatuwakilishe vizuri,” alisema Ndyariagije.Simba bado ipo Dodoma na leo inatarajiwa kulipeleka kombe hilo Bungeni, kufuatia mwaliko waliopewa na wabunge wanaoishabikia timu hiyo na baada ya hapo uongozi utatoa taarifa kuhusu kitakachofuata kama kurudi Dar es Salaam au kwingineko.
4
RAYMOND MINJA IRINGA Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Muslim ametoa onyo kali kwa madereva wa mabasi  kuacha tabia ya kukimbiza magari  kwa spindi kubwa hali  inayohatarisha usalama wa abiria na kwamba wakishindwa kufanya hivyo leseni zao zitafungiwa au kufutwa. Onyo hilo limekuja ikiwa ni siku chache tangu kuonekana kwa kipande cha video ya magari mawili ya kampuni ya Happy Nation na Rugwe yakionekana kushindana kukimbia bila ya kujali usalama wa abiria waliowabeba. Akizungumza na madereva wa mabasi yaendayo mikoani kwenye stendi ya mabasi Igumbiro mkoani Iringa, Muslim alisema kuwa hatofumbia macho wala kuvulimia Watanzania wakipoteza Maisha kutokana na uzembe wa dereva. Muslim alisema kuwa hadi sasa madereva 13 wameshafungiwa na wengine  kufutiwa leseni zao kutokana na makosa mbalimbali  ya barabara na kuwataka madereva kutii sharia bila shuruti ili kulinda ugali wao. Alisema kuwa hivi sasa kumekuwa na tabia ya madereva kubeti na mabosi wao kuwa ni nani atawahi kufikasha basi kwa haraka  kwenye mkoa anaokwenda jambo ambalo linamchochea kuendesha gari kwa spidi kubwa ili awahi kufika na kuchukua fedha yake. Aidha amewataka watu wa vikosi vya usalama barabarani kote nchini kuhakikisha wanawakamata na kuwafungia au kuwafutia  lesini madereva wote watakaokiuka sheria za usalama barabarani ili kunusuru maisha ya Watanzania wasiokuwa na hatia.
3
WADAU mbalimbali wa soka nchini wamesema Tanzania inaweza kufuzu fainali zijazo za Afrika, Afcon iwapo hakutakuwa na ubabaishaji wa maandalizi ya kikosi hicho mapema.Katika ratiba iliyotolewa juzi na Shirikisho la soka Afrika (CAF), Tanzania imepangwa kundi J, lenye timu za Tunisia, Libya na Guinea ya Ikweta. Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wadau hao walisema kinachohitajika kwa sasa ni maandalizi mazuri na kuwa makini kwa kuweka mipango mapema.“Tukifanya maandalizi mazuri tutakuwa na nafasi lakini tukiendelea na ubabaishaji hatuwezi kufika popote. Wahusika wanatakiwa kuandaa utaratibu mzuri na yote yanawezekana,”alisema mchezaji wa zamani wa Simba na Yanga Zamoyoni Mogella.Mogella alisema kunahitajika mechi zenye nguvu za kujipima nguvu, uchaguzi bora wa wachezaji na benchi la ufundi na mipango. Mchambuzi wa soka Ally Mayay alisema kundi la Tanzania sio jepesi kwasababu Tunisia na Libya ni timu nzuri ambazo kama hakuna maandalizi bora ya kuwakabili zinaweza kuwa ngumu.Mchezaji huyo wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, alisema kinachohitajika ni kampeni za hamasa kuanza mapema za kushinda angalau mechi mbili za nyumbani kutoka kwa Libya na Guinea ya Ikweta na kugawana pointi na Tunisia.Kingine alisema ni lazima mipango ianze sasa kwa maana ya kuwepo na kikosi kipana chenye nguvu kitakachomsaidia kocha kuelekea kwenye michuano hiyo sambamba na ile ya CHAN (Kombe la mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani).Mchambuzi mwingine wa soka, Dominiki Salamba alisema kundi sio jepesi na kwamba anaona changamoto kubwa itakuwepo zaidi katika michezo ya ugenini na kutaka mipango na umakini uwepo katika maandalizi.Alisema wachaguliwe wachezaji wanaostahili bila kuangalia watu, lakini kingine akisisitiza litafutwe benchi la ufundi ambalo litakaa na wachezaji kwa muda mrefu na kuwasoma.Salamba alisisitiza pia, vijana wanaocheza ligi za ndani waendelee kuaminiwa na kupewa nafasi kwenye kikosi hicho ili kujiuza na kupata nafasi ya kucheza soka nje ya nchi.Kocha wa zamani wa Taifa Stars Charles Mkwasa alisema kundi ni gumu kulingana na wapinzani waliopo kwa kuwa, Taifa Stars hutegemea zaidi wachezaji wa ndani ukilinganisha na wengine huku akihimiza ligi zitengeneze mfumo utakaowezesha kuzalisha wachezaji wenye uwezo wa kushindana.
4
Na HAMISA MAGANGA, UTAFITI uliofanyika hivi majuzi umebaini kuwa kumaliza tatizo la ndoa za utotoni kunaweza kusaidia nchi zinazoendelea kukuza uchumi kwa kuongeza mabilioni ya dola za Marekani. Hii ni kwa kupunguza kasi ya ukuaji wa idadi ya watu waliotegemezi, kuboresha elimu na afya kwa wasichana wadogo na watoto wao, kupunguza bajeti za serikali na kuongeza uwezo wa wanawake kujiongezea kipato. Ndoa za utotoni ni chanzo cha matatizo mbalimbali ya kijamii ikiwamo afya na kukosa elimu kwa wasichana wenyewe, ambapo tatizo hili pia huwakumba watoto wao na kizazi chao kwa ujumla. Wakati idadi ya wasichana walio chini ya umri wa miaka 18 wanaoolewa ikipungua katika miaka ya hivi karibuni, ikiwa ni mpango wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kukomesha ndoa za utotoni, juhudi hizo zimekwama katika nchi nyingi za Kiafrika na Kusini mwa Asia. Katika nchi hizo, ndoa za utotoni zimeshamiri. Mfano, nchini Niger asilimia 77 ya wasichana wenye umri kati ya miaka 18 na 22 wameolewa licha ya kuwapo mikakati mingi ya serikali kuondoa hali hiyo. Hali ilivyo duniani ni kwamba wasichana zaidi ya milioni 15 kila mwaka wanaolewa kabla ya umri wa miaka 18. Wanaharakati wanaopinga ndoa za utotoni wanasema Jumuiya ya Kimataifa inahitaji kutafuta njia mbadala za kumaliza tatizo hilo. Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa zaidi ya wanawake milioni 700 duniani waliolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18, zaidi ya theluthi moja waliolewa kabla ya miaka 15. Iwapo hatua madhubuti hazitachukuliwa, idadi ya ndoa za utotoni hasa katika nchi za Afrika zitaongezeka. Hivyo, Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa ifikapo mwaka 2050 wasichana wengi walio chini ya miaka 18 watakuwa majumbani bila shughuli zozote za kijamii. Ukweli ni kwamba, uwekezaji katika kumaliza ndoa za utotoni bado unasumbua nchi nyingi duniani. Ripoti mpya ya athari za kiuchumi zinazotokana na ndoa za utotoni iliyotolewa wiki iliyopita na Benki ya Dunia (WB) na Kituo cha Kimataifa cha Utafiti juu ya Wanawake (ICRW) imebainisha hali hiyo. Utafiti huo unatoa makadirio mapya ya kitaifa na kimataifa kwa kiasi cha fedha ambacho kinaweza kuokolewa iwapo tatizo hilo litakwisha. “Ndoa za utotoni si tu zinaathiri matumaini na ndoto za wasichana, bali piahuzuia juhudi za kukomesha umasikini na kufikia ukuaji wa uchumi na usawa,” anasema Quentin Wodon ambaye ni Mkurugenzi wa Mradi wa WB na mwandishi mwenza wa ripoti hiyo. Anasema; “kumaliza tatizo hili si tu jambo la haki na kimaadili, bali pia linalenga suala zima la kukuza uchumi.” Ripoti hiyo inatoa mfano kwamba nchini Niger faida inayoweza kupatikana kwa kupiga marufuku ndoa kwa watoto waliochini ya miaka 18 itafikia Dola za Marekani bilioni 1.7 ifikapo mwaka 2030; wakati nchini Ethiopia itakuwa Dola za Marekani bilioni 4.8 na karibu Dola za Marekani bilioni moja kwa upande wa Nepal. Hiyo inatokana na utafiti kuonesha kuwa wasichana wanaoolewa wakiwa na umri wa miaka 13  kwa ujumla wake- wana uwezekano wa kuongeza asilimia 26 zaidi idadi ya watoto wanaozaa kulinganisha na wale wanaoolewa wakiwa na umri wa miaka 18 au zaidi na hivyo kuongeza idadi ya watu tegemezi na madeni makubwa kwa serikali. Zaidi ya hayo, katika ngazi ya kimataifa, utafiti huo unabainisha kuwa iwapo ndoa za utotoni zingekoma mwaka 2015, uchumi wa dunia ungeongezeka kwa Dola za Marekani bilioni 566 ifikapo 2030; hii ni kutokana na nguvu kazi ambayo ingekuwapo. Sasa basi, tafiti mbalimbali zinahitajika ili kubaini gharama zinazotokana na ndoa za utotoni katika nchi zilizoendelea kama Marekani, ambako pia wanakabiliwa na tatizo hili, pamoja na nchi masikini ambako hali ni tete zaidi. Uchunguzi mpya wa ICRW na Utafiti wa WB, pia umebaini kuwa asilimia kubwa ya watoto walioolewa walilazimika kuacha masomo yao na hivyo kukatisha ndoto zao za kimaendeleo. Ndoa za utotoni pia zinahusishwa na matukio ya vifo vya watoto chini ya miaka 5 na hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa husika. Ripoti hiyo inaongeza kuwa maboresho katika umiliki wa ardhi, ushiriki wa wanawake katika uamuzi, pamoja na kupunguza unyanyasaji wa kijinsia – mambo ambayo yanachangiwa kwa namna moja au nyingine na ndoa za utotoni, yanaweza kusaidia kukuza uchumi wa nchi. “Matokeo ya gharama za kiuchumi yatasaidia kuleta majadiliano kuhusu kumaliza ndoa za utotoni katika nchi zinazoendelea,” anasema Lakshmi Sundaram, Mkurugenzi Mtendaji wa Wasichana wasioolewa. “Baadhi ya watu wanadhani kuwa ndoa za utotoni haziligharimu chochote taifa, lakini ripoti hii inaweka wazi ukubwa wa tatizo na mabilioni na trilioni za dola zinazopotea… hii inaweza kufungua majadiliano kwanini ni muhimu kwa wasichana kufanya uamuzi kuhusu maisha yao,”anasema. Naye Mkurugenzi wa Mradi wa ICRW na mwandishi mwenza wa ripoti hiyo, Suzanne Petroni anasema: “Umaskini, ukosefu wa usawa wa kijinsia, upatikanaji duni wa elimu bora, ukosefu wa huduma za afya ya uzazi, ukosefu wa fursa za ajira, kusaidia kuendeleza ndoa za utotoni na kuzaa kabla ya umri ni miongoni mwa mambo yanayochangia kudumaza uchumi.” Hali ilivyo Tanzania Suala la ndoa za utotoni Tanzania limesababisha idadi kubwa ya wasichana wenye umri chini ya miaka 18 kukatisha masomo yao. Mwaka jana, Shirika lisilokuwa la kiserikali la Plan International lilifanya utafiti na kugundua kuwa nafasi ya watoto wa kike ulimwenguni haionekani machoni pa watu. Liligundua kuwa takwimu zinazowahusu watoto wa kike ziko nyuma ya wakati, hazijakamilika na wakati mwingine mapendekezo ya tafiti zake hayafanyiwi utekelezaji. Hapa nchini imeonekana hakuna takwimu sahihi zinazoonyesha uhalisia wa changamoto anazozipata mtoto wa kike kutokana na ndoa za utotoni, hivyo kusababisha thamani yake kushuka katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo ambapo madhara yake huonekana baadae akiwa mtu mzima. Akitoa ripoti hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi wa Mtoto kutoka shirika hilo kwa upande wa Tanzania, Jane Mrema anasema kiwango cha ndoa za utotoni kwa Tanznia kimefikia asilimia 36 ambacho ni kikubwa zaidi ya kiwango cha Dunia cha asilimia 34 na kwa hesabu za kimkoa ni asilimia 59 kwa kila mkoa. Utafiti huo ulifanyika kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na mashirika yasiyo ya kiserikali likiwamo Plan International, Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Shirika linalohusiana na Utafiti na maendeleo ya Afya ya Wanawake (FORWARD) na Shirika la Utafiti juu ya Kupunguza Umasikini (REPOA). Ripoti ya utafiti huo ulioitwa Visababishi na Madhara ya Ndoa za Utotoni Nchini Tanzania, ulionyesha kuwa umasikini ndio sababu kubwa ya kuwapo kwa ndoa za utotoni. Baadhi ya mikoa ambayo wananchi walihojiwa wakati wa utafiti wamekubali kwa nguvu zote kuwa fedha zinazolipwa kwa ajili ya mahari ndizo zinazowasababisha kuwaoza watoto wao wakiwa bado wadogo. Utafiti huo unaonesha Mkoa wa Mara wananchi asilimia 59 wanakubalina na majibu ya utafiti huo wakati jijini Dar es Salaam asilimia 56, Dodoma asilimia 53, Lindi asilimia 52 na Tabora asilimia 51. Sababu nyingine ya ndoa za utotoni ni mtazamo wa tamaduni, mila na desturi baina ya jamii mbalimbali kuhusu miaka ya mtoto wa kike anayetakiwa kuolewa, unyago, ukeketaji pamoja na ngoma za asili zinazochangia watoto kuozwa mapema. Tafiti hizo zinaonyesha kuwa maeneo ya vijijini asilimia 18 ya wanawake wamekeketwa wakati mijini ni asilimia saba na mikoa inayoongoza na asilimia yake kwenye mabano ni Manyara (81) Dodoma (68), Arusha (55), Singida (43) na Mara (38). Aidha, asilimia 24 ya waliohojiwa mkoani Shinyanga na asilimia 20 mkoani Tabora wamesema mikoa hiyo ina kiwango kikubwa cha ndoa za watoto walio na umri chini ya miaka 18. Utafiti huo pia umegundua kuwa ukosefu wa elimu unasababisha wasichana kuingia kwenye ndoa wakiwa bado wadogo kiumri, hii inatokana na kushindwa kuendelea na masomo baada ya kumaliza elimu ya msingi ama kukatisha kabisa masomo yao kabla ya kuhitimu. Kutokana na utafiti huo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Plan International- Tanzania, Jorgen Haldorsen anasema: “Matokeo ya utafiti huo yanawapa mwongozo wa kujua sehemu zilizoathirika zaidi ili kuweka nguvu za kutosha na kufahamu namna mbalimbali za kutumia kuwafikia waathirika hao.” Naye Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu anasema anapinga kwa vitendo ndoa na mimba za utotoni kwa kuwa ni changamoto kwa maendeleo ya Tanzania. “Tunataka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, lakini hatutaweza kuwa na nchi yenye viwanda wakati watoto 36 katika kila watoto 100 nchini wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18 na watoto 27 wa Kitanzania wanapata mimba kabla ya umri huo, hili ni tatizo kubwa ambalo athari zake zitaonekana baadaye”anasema Ummy. Katika kuhakikisha ndoa hizo zinakoma, ameanza kutumia marekebisho ya Sheria ya Elimu yaliyopitishwa na Bunge Juni 2016 ambayo yanakataza mtu yoyote kumuoa mtoto wa shule ya msingi au sekondari kwa kuwa ni kosa la jinai lenye adhabu ya miaka 30 jela. Pia, amewataka maafisa maendeleo ya jamii wa kila halmashauri kupita nyumba kwa nyumba kuwaibua wazazi wanaofanya vitendo hivyo na kuwasilisha taarifa hizo sehemu husika ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sheria hiyo. Viongozi wa dini nao wanasisitiza suala la kusomesha watoto wa kike ili waweze kufahamu mabaya na mazuri hatimaye wajiepushe na vitendo viovu vikiwamo vya kudanganywa na kuingia katika mapenzi wakiwa na umri mdogo. Pia wanashauri kuangalia utaratibu wa kuwalea watoto wanaoishi katika mazingira magumu ili nao waje kuwa wanawake wanaoweza kuleta maendeleo katika taifa lao. Hata hivyo, ili kulimaliza suala hili ni muhimu wazazi kuelimishwa juu ya madhara ya ndoa za utotoni. Mimba za utotoni nazo juu Takwimu zinaonesha kuwa tatizo la mimba za utotoni nchini limeongezeka kutoka asilimia 23 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 27 mwaka 2016/17. Sababu kubwa inatajwa kuwa ni ukosefu wa huduma pamoja na elimu ya afya ya uzazi kwa vijana wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 19. Takwimu hizo zilitolewa hivi karibuni na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Vijana- Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Venerose Mtenga wakati akizindua mradi wa ‘AMUA Innovation Accelerator, Sexual and Reproductive Health Challenge.’ Anasema: “Tatizo hili ni kubwa, mimba za utotoni bado changamoto hasa kwa vijana wa vijini kutokana kwamba hawajafikiwa na huduma au elimu ya afya ya uzazi.” Naye Kaimu Mkurugenzi wa Afya ya Mama na Mtoto kutoka Wizara ya Afya, Dk. Felix Bundala anasema tatizo la mimba za utotoni limechangia kuongezeka kwa vifo vya kina mama na watoto ambapo kwa sasa takwimu zinaonyesha kuwa kati ya vizazi 100,000 kina mama zaidi ya 550 hupoteza maisha wakati kati ya watoto wachanga 1,000 watoto 25 hufariki dunia.
0
MWANDISHI chipukizi wa miswada (script) anayeandika kwa kutumia ulimi, Wakonta Kapunda, amesema baada ya kumaliza mafunzo ya uandishi wa script, Bodi ya Filamu nchini imeahidi kumpa kazi ya kuandika script za filamu mbalimbali. “Watendaji wa Bodi ya Filamu na Chama cha Wasanii wa Filamu (Taff), walikuja kunijulia hali akiwemo mkurugenzi wa bodi hiyo waliniahidi kwamba baada ya kumaliza mafunzo yangu watanipa kazi ya kuandika script za filamu mbalimbali nimefurahi kwa kweli kama watanipa kazi hizo,” alieleza. Wakonta anasema kutokana na kuwa mwangaliaji wa filamu mzuri amegundua kwamba filamu zinabadilisha maisha ya wengi na zinaongeza faraja na kujenga kujiamini kwa maisha mapya ndiyo maana naye anataka kuwa mwandishi wa hadithi za kuleta faraja kwa kuwapa watu imani ya kuwa na maisha ya kutokata tamaa hata baya likiwakuta. “Filamu ni maisha, inaweza kumjenga mtu kumliwaza na kumweka sawa kutoka kwenye majonzi, mimi nilikuwa mwangaliaji mkubwa wa filamu, nilikuwa nikiangalia zaidi waandishi wa script kutoka nje ya nchi na huko nilijifunza baadhi ya vitu lakini nilipokuja kwenye mafunzo ufahamu wangu wa uandishi ukaongezeka nashukuru kwa hilo na naona ndoto yangu inaelekea kutimia,” alieleza. “Changamoto yangu kubwa kwa sasa ni vifaa vya kuandikia, natumia simu hii (anaonyesha) lakini pia ningepata baiskeli ya umeme ingenirahisishia zaidi kuliko hii ya kusukumwa wakati mwingine anayenisukuma huchoka,” alieleza Wakonta.
1
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza  hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi.  Kwa misingi kama hiyo sisi kama  chombo cha habari  tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk.  Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia.  Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”.  Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi,  Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii.  Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo.  Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge.  viongozi  wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo.
5
Zainab Iddy, Dar es Salaam BAADA ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kutangaza ligi zitachezwa bila mashabiki kutokana na tishio la virusi vya Corona, Serikali kupitia Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Yusuph Singo, amelitaka shirikisho hilo kutokurupuka na badala yake kufuata maagizo yatakayotolewa na mamlaka husika. Hivi karibuni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alitangaza kusitisha shughuli zote zinazoleta mkusanyiko ikiwamo michezo kwa siku 30 kuanzia Machi 18, mwaka huu, ili kupunguza ongezeko la janga la Corona nchini. Akizungumza na MTANZANIA juzi, Singo alisema wizara ilisikia kile kilichozungumzwa na TFF, lakini walifanya haraka kutoa uamuzi kabla ya kujua kipi ambacho serikali itasema baada ya siku 30 kumalizika. “Baada ya siku 30 zilizotolewa na Serikali kumalizika, wizara husika itakuja na taarifa ambayo ndivyo itakayotoa mwongozo kulingana na hali ya ugonjwa wa Corona itakavyokuwa kipindi hicho. “Inaweza ligi kuendelea au kutoendelea, kama itaendelea vipi itafanyika, wizara ndiyo itakayozishauri mamlaka husika, kilichozungumzwa na TFF ni mapema mno,” alisema. Singo aliongeza: “Zuio la siku 30 limeigusa michezo mingi kwani katika soka mbali na ligi kulikuwa na timu za taifa, lakini pia bado kuna michezo iliyokuwa ikijiandaa na Olimpiki na mashindano mengine mengi yote hiyo itapewa mwongozo jinsi gani watakavyoendelea na shughuli zao kama itabidi kuwa hivyo.”
4
Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA SHIRIKA la Viwango Nchini (TBS) limeomba msaada kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Maji na Mifugo wa jinsi ya kukabiliana na uingizwaji wa nguo za ndani za mitumba nchini. Ombi hilo lilitolewa jijini hapa na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk. Yusuph Ngenya alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli zinazofanywa na shirika hilo kwa Kamati ya Kilimo, Maji na Mifugo. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Stela Manyanya. Hoja ya nguo za ndani iliibuliwa na mjumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa (CCM) ambaye alitaka apewe majibu ni kwanini bado nguo za ndani zimeendelea kuingizwa nchini licha ya Serikali kukataza. “Nguo za ndani zinatupa shida sana, tunaomba mtusaidie, zinaingizwa kwa kufichwa,” alisema Ndassa. Akimjibu, Dk. Ngenya alisema wamekuwa wakifanya jitihada za kuhakikisha mitumba ya nguo za ndani kama chupi na zingine haziingii nchini. Alisema wafanyabiashara wamekuwa wakiziingiza nchini kwa kuchanganya na nguo zingine hali ambayo imekuwa ikiwapa wakati mgumu kubaini. “Wanazificha kwa kuziweka ndani ya nguo za kawaida, naomba mtusaidie, naomba msaada wa kamati kuhusiana na nguo za ndani, hebu hili tusaidieni,” alisema Dk. Ngenya. Alisema katika kipindi cha miaka minne, TBS imekusanya viwango 1,600 katika sekta mbalimbali sawa na asilimia 108.5  “Mafanikio tumefanikiwa ujenzi wa jengo jipya la maabara ya kisasa ambalo litarahisisha utendaji kazi pamoja na urahisishaji wa vipimo,” alisema Dk. Ngenya. Alisema mwaka 2016/17 hadi Desemba 2019  shirika limetoa gawio kwa Serikali Sh bilioni 36.4. Dk. Ngenya alisema kwa sasa mambo yote yanaenda kwa mtandao na hakuna urasimu wala rushwa katika utendaji kazi wa shirika hilo. Alisema kumekuwapo na ushirikiano kati ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani katika mambo mbalimbali. Dk. Ngenya alisema wanakabiliwa na changamoto ya ongozeko la njia zisizo rasmi pamoja na uhaba wa vifaa vya kisasa kwa maabara. “Tumekuwa tukifanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maeneo ya mipakani na tumeanzisha vituo vya ukaguzi na tumeongeza pale Tarakea na maeneo mengine. “Tumeendelea kununua vifaa vya kisasa ili kuleta tija, lakini pia tumekuwa tukisaidiwa na wadau wa maendeleo,” alisema Dk. Ngenya. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda na Biashara, Mahmood Mgimwa, ambaye alikuwa mgeni mwalikwa kwenye kikao hicho, alisema TBS inatakiwa itoe elimu ya kutosha ili wananchi waweze kuijua. “Mmesema changamoto mnayokabiliana nayo ni kuwepo kwa njia za panya, sasa mbona hamjasema kwamba mna uhaba wa watumishi ili wawasaidie kuzuia hizo njia za panya, lazima ‘one stop centre’ (kituo cha pamoja cha huduma) ijengwe,” alisema Mgimwa.
3
WAKIMBIZI wa Sudan Kusini wanaoishi katika kambi ya Nyumanzi iliyopo katika mpaka wa Uganda na nchi hiyo, wamemuomba Rais wa Tanzania, John Magufuli na Watanzania wote kusaidia kurejesha amani nchini mwao.Ombi hilo walilitoa hivi karibuni kupitia kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian Tanzania, Emmaus Mwamakula alipofanya ziara katika kambi hiyo kwa ombi la wakimbizi, ikiwa ni sehemu ya safari yake ya kitume Sudan Kusini.Kwa mujibu wa Askofu Mwamakula, kambi hiyo inahifadhi takriban wakimbizi 50,000.Askofu Mwamakula ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani, katika taarifa yake aliyoituma kwa njia ya mtandao wa kijamii, alisema wakimbizi hao walielezwa kuguswa na uongozi wa Rais Magufuli kwa namna anavyosimamia haki za wanyonge na kueleza kuwa wana matumaini anaweza kuwasaidia.“Nilikuwa na ziara ya kihuduma Jambio na Juba, Sudan Kusini, lakini safari yetu ya kitume ilibadilika ghafla baada ya kupokea ombi kutoka kwa wakimbizi wa Nyumanzi waliotuomba tuwatembelee katika kambi yao tuwasikilize na kujionea hali halisi kabla ya kuendelea na safari,” alisema Askofu Mwamakula.Alisema Machi 22, mwaka huu alifika katika kambi hiyo akiwa na Askofu wa Kanisa la Moravian la Uamsho nchini Uganda, Odongo Mario Arabous na kupokewa na maaskofu watatu wa Anglikana ambao ni wakimbizi na walifanya ibada kabla ya kuwasikiliza.“Maaskofu wale (watatu wakimbizi) walinipa ujumbe mzito wakiwawakilisha wakimbizi wenzao wakiamini nitawasaidia kuufikisha kwa Rais Magufuli na viongozi wengine duniani, kwamba wanatamani amani nchini mwao ili warejee,” alisema Mwamakula.Alisema maaskofu hao pamoja na kumshukuru Rais Yoweri Museveni wa Uganda kwa kuwahifadhi nchini mwake, wanaamini kuwa sauti ya Rais Magufuli na Tanzania kwa ujumla itasaidia sana kutatua mgogoro wa Sudan Kusini.Askofu Mwamakula alisema alifanikiwa pia kukutana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Sudan Kusini, John Machar ambaye naye ni mkimbizi anayeishi Nakuru nchini Kenya baada ya kumfuata Nakuru kwa mwito wa kukutana naye ili kusisitiza hitaji lao la kuomba amani nchini mwao (Sudan Kusini).“Waliniunganisha na maaskofu wengine walioko Marekani na Australia kwa mkutano wa simu (phone conference) na kwa hakika wote wametamani Rais Magufuli awasaidie kupaza sauti itakayosaidia kurejesha amani nchini mwao ili warudi na kuendelea na maisha yao kama nchi nyingine,” alisema.Julai 9, 2011 Sudan Kusini ilijitenga rasmi na Jamhuri ya Sudan na kuwa Taifa huru. Hata hivyo, iliingia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013 baada ya Rais Salva Kiir kumshutumu Makamu wake (wakati huo), Riek Machar kuwa anafanya majaribio ya kumpindua.Machafuko hayo yamesababisha mamia ya watu kupoteza maisha na maelfu kuyakimbia makazi yao.
3
OSCAR ASSENGA-TANGA ALIYEKUWA Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano katika Serikali ya Awamu ya Nne, Omari Nundu ametangaza nia ya kuwania ubunge Jimbo la Tanga Mjini, mwaka 2020 pindi CCM itakapotangaza utaratibu rasmi. Amesema baada ya chama hicho tawala kutangaza utaratibu rasmi atachukua fomu na kuirudisha ili kuomba ridhaa ya chama hicho. Kauli hiyo aliitoa jana jijini Tanga, katika hafla ya kukabidhi vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya vilivyotolewa na wadau wa maendeleo kupitia mitandao ya kijamii ya WhatsApp. Nundu aliwahi kuwa mbunge wa jimbo hilo mwaka 2010 hadi 2015 alipopigwa mweleka wa kushindwa na Mbunge wa sasa, Mussa Mbaruku (CUF). “Labda niwaambie kwamba ikifika mwaka 2020 wakati wa kugombea nitachukua fomu, nitazijaza na kugombea, lakini kwa sasa hamtoniona nikigawa fedha kwa watu elfu ishirini ishirini wala futari. “Nimesikia maneno mtaani yanapita kwamba Nundu anataka kugombea ubunge, niwaambie kwamba ikifika mwaka 2020 wakati ukifika na chama kikitangaza utaratibu wake, nami nitajitosa, lakini si sasa jamani, chama bado hakijasema ndugu zangu,” alisema Nundu. Alisema katu hawezi kutoa fedha kwa watu ila atashiriki kila hatua katika shughuli za maendeleo ya Jimbo la Tanga na mkoa mzima.  “Nitasimamia suala la maendeleo mpaka hatua ya mwisho, sasa tuna rais (Dk. John Magufuli) ambaye anasaidia na kusukuma maendeleo kwa kasi kubwa kwani matunda yake yameonekana kwenye sekta mbalimbali,” alisema. Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Daudi Mayeji, aliwashukuru wote waliochangia vifaa hivyo vya matumizi ya hospitali na kusema sasa watakuwa wanapokea vifaa kwa utaratibu wa kiserikali. Mayeji alisema kwamba wao Serikali wanapokea misaada yoyote ile hasa isiyo na masharti na wanaingiza kwenye matumizi, kwamba hawana sababu yoyote ya kukataa kitu ambacho kimekuwa kikitolewa na wadau.
3
JESHI la Polisi mkoani Dodoma linawashikilia watuhumiwa 44 kwa kufanya makosa mbalimbali ya uhalifu, wakiwemo 10 waliochoma moto nguzo 82 za Mradi wa Umeme Vijijini (REA) na kati yake 55 kuteketeza kabisa.Watuhumiwa wa kuchoma nguzo hizo zenye thamani ya Sh milioni 15.125, walikamatwa Oktoba 2 mwaka huu, katika kijiji cha Makang’wa, kata na tarafa ya Makang’wa wilayani Chamwino mkoa wa Dodoma.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto alisema nguzo hizo ni za mradi wa kusambaza umeme huo unaotekelezwa na mkandarasi wa Kampuni ya Derm Electric. Kamanda Muroto alisema katika msako unaoendelea jijini hapo, Jeshi la Polisi pia liliwakamata watuhumiwa 29 wa udhalilishaji wa kijinsia na ukiukaji wa maadili, wakiwemo makahaba wanawake 22, wanaume watano na waendesha madanguro wanne.Katika msako huo, pia jeshi hilo liliwakamata watuhumiwa Sylvester Malolo (24) mkazi wa Chinangali, John Lusamba (21) mkazi wa Mailimoja, wakiwa na mali za wizi ambazo ni televisheni tatu, redio mbili na laptop baada ya kuvunja klabu ya Free point iliyopo eneo la Uhindini. Kati yao, mtuhumiwa Lusamba alikuwa gerezani na alitoka Septemba mwaka huu.Hata hivyo mtuhumiwa wa tatu, Gerald Mwaisumo alitoroka na Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka. Pia jeshi hilo lilimkamata John Victory (19) mkazi wa Farkwa wilayani Chemba akiwa na nyama kilo 4.5 ya swala iliyowindwa bila kibali wakati hiyo ni nyara ya serikali.Katika tukio lingine, Jeshi la Polisi Oktoba 6 mwaka huu, lilikamata wahamiaji haramu wanne, waliokuwa wakisafiri na basi la Hajis Line Up lenye namba za usajili T 298 DCH kutoka Arusha kwenda Mbeya.Aliwataja wahamiaji hao kuwa ni Abdul Musa (26) raia wa Somalia na Migafu Gezehani (18) raia wa Ethiopia, Abdi Mohamed na Mohamed Dai wote raia wa Somalia ambao walikamatwa katika stendi ya mabasi jijini Dodoma eneo la Nanenane. Wote watafikishwa mahakamani upelelezi ukikamilika.Katika tukio lingine, Oktoba 7 mwaka huu, jeshi hilo lilimkamata mtuhumiwa Maloga Sanja(41) katika kijiji cha Chitemo wilayani Mpwapwa akiwa na silaha aina ya gobori likiwa na risasi 16 zilizotengenezwa kienyeji.
3
Na ZAINAB IDDY-DAR ES SALAAM KAMA ulikuwa unafikiri Simba ni timu ya mchezo, basi utakuwa umekosea, kwani hivi sasa Wekundu hao wa Msimbazi hawataki mzaha kabisa, baada ya kubainisha kuwa wanahitaji mafanikio kama ya klabu ya TP Mazembe ya Congo. Hadi mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu unamalizika, Simba wameweza kumaliza wakiwa nafasi ya kwanza, baada ya kufikisha pointi 35 katika michezo 15, ambapo wamepoteza mechi mbili pekee na hivyo kuwa mbele ya watani zao, Yanga, wenye pointi 32 nafasi ya pili. Akizungumza na MTANZANIA Jumapili, Meneja wa kikosi hicho, Mussa Hassan ‘Mgosi’, alisema katika usajili wa dirisha dogo, wanahitaji wachezaji wanaojituma na watakaohakikisha Simba inatwaa ubingwa kwa kushirikiana na wale watakaowakuta. Alisema kocha wao, Joseph Omog, wengi wanamjua kuwa ni muumini wa soka la kisasa linalomtaka kila mchezaji kuwa na maamuzi ya haraka pindi akiwa na mpira miguuni na kwa kuwa kikosi chao tayari kimeshaingia kwenye falsafa hiyo, hata wale watakaobahatika kuongezwa katika dirisha dogo la usajili ni lazima waendane na mfumo huo. “Hatufanyi usajili kishabiki wala kukomoana, kwetu tutaongeza wachezaji kulingana na matakwa ya benchi la ufundi, lakini lazima hao wanandinga wawe wazuri zaidi ya waliokuwepo kikosini hivi sasa, ili nao wawe wepesi wa kuingia katika falsafa ya Kocha Omog ya soka la kisasa. “Soka la kisasa linamtaka kila mchezaji kucheza kwa kujiamini na kisha kutumia nafasi atakayoipata vizuri ili kuisaidia timu kupata ushindi, ndiyo maana kocha Omog mara nyingi awape mbinu za kisasa  wanandinga wake kwa kuwa anajua licha ya kuhitaji ubingwa lakini inahitaji mafanikio kama yaliyofikiwa na TP Mazembe,” alisema. “Kwa hivi sasa mpira wa miguu umebadilika, hivyo lazima Simba iwe na wachezaji wanaojitambua na kujua majukumu yao ndani ya timu, kila mmoja kutumia akili na kufanya maamuzi ya haraka, lakini pia ni lazima wakati wote wawe mchezoni ili ikitokea amepata mpira ajue anaupeleka wapi kwaajili ya kuchangia ushindi wa timu,” alisema. Kwa mujibu wa taarifa ambazo MTANZANIA Jumapili linazo, ripoti ya kocha imeitaka Simba iachane na wachezaji saba ambao wameonekana kutokuwa na msaada kwenye mzunguko wa kwanza, lakini pia ikihitaji kusajiliwa kwa wachezaji watatu katika nafasi ya mshambuliaji, beki na kipa atakayesaidiana na Vincent Angban.
4
Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Beng’i Issa amesema waratibu hao wana wajibu wa kuhakikisha wanatumia ujuzi walioupata kwa faida ya wananchi katika mikoa yao. Jumla ya waratibu 41 wa madawati ya uwezeshaji kutoka katika mikoa ya Ruvuma, Iringa, Njombe, Rukwa, Songwe na Mbeya walipatiwa mafunzo ya siku tatu jijini Mbeya.Mafunzo hayo yalimalizika mwishoni mwa wiki. “Tumewapatia mafunzo waratibu hawa wakafanye kazi kwa niaba ya baraza kutekeleza sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi,” alisema.Alisema mafunzo hayo yamelenga kuwapatia ufahamu wa kujua wajibu wao, kufanya kazi na jamii, kuibua fursa, kuwaonyesha fursa wananchi na kuwaunganisha na vyombo vya fedha na mifuko ya serikali kupata mikopo kuendeleza shughuli za kijasiriamali.Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa NEEC, mafanikio na changamoto zitakazojitokeza katika kanda hiyo zitatumika katika kuboresha kanda nyingine zilizobaki.Alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imeweka kipaumbele katika kuwawezesha wananchi kiuchumi hivyo kupitia waratibu hao wananchi watafikiwa kwa wingi na urahisi.Kaimu Katibu Tawala, mkoa wa Mbeya, Nyasebwa Chimagu alisema waratibu hao wamepatiwa dhamana kubwa na serikali hivyo wakatumike katika kupeleka elimu kwa wananchi juu ya uwezeshaji.Mratibu wa dawati la uwezeshaji, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Pelisius Kalikule alisema ameyapokea vizuri mafunzo hayo na amejipanga kwenda kufanya kazi aliyopewa na serikali.
5