text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
BARCELONA, HISPANIA KIVUMBI cha michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kinatarajia kuendelea leo hatua ya robo fainali baada ya michezo mingine kupigwa jana, leo Barcelona watakuwa kwenye uwanja wa nyumbani na kuwakaribisha wapinzani wao Man United ambao waliwachapa kwenye fainali mbili. Huu ni moja kati ya michezo ambayo itakuwa ya kisasi kutokana na historia ya nyuma walivyokutana, Barcelona wamekuwa wababe wa wapinzani hao hasa kwenye hatua hizo za juu kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya. Barcelona waliwachapa Man United mwaka 2009 katika fainali ya michuano hiyo kwa ushindi wa mabao 2-0, yaliwekwa wavuni na Samuel Eto’o na Lionel Messi na kutwaa ubingwa huo. Msimu uliofuata Barcelona waliendeleza ubabe wao kwa kutwaa ubingwa huo kutokana na ushindi wa mabao 3-1, huku mabao hayo yakifungwa na Messi, Pedro Rodriguez pamoja na David Villa, wakati huo bao la Man United likifungwa na Wayne Rooney. Wachezaji waliobaki ndani ya Barcelona ambao waliongoza katika safu ya ushambuliaji na kupata mabao hayo, amebakia Messi ambaye alifunga katika fainali zote mbili walizokutana na leo wanakwenda kukutana kwenye robo fainali. Kumbukumbu zinaonesha timu hizo zimekutana mara 11 katika historia yao, huku Man United ikishinda mara tatu, lakini Barcelona wamekuwa wababe zaidi. Messi amefunga jumla ya mabao 22 ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, akizifunga timu za England na kuwa mchezaji wa kwanza kuwa na mabao mengi ya michuano hiyo kwa kuzifunga timu hizo za England. Mchezo huo unaweza kumpa heshima kubwa kocha wa Man United, Ole Gunnar Solskjaer, endapo United itafanya vizuri. Kocha huyo alipewa jukumu hilo tangu Desemba mwaka jana akichukua nafasi ya Jose Mourinho, lakini kitendo hicho cha kupangiwa Barcelona ambao wamekuwa na uzoefu mkubwa wa michuano hiyo, kinaonekana kama ndio mwisho wa Man United japokuwa waliishangaza dunia kwa kuwaondoa wababe wa soka nchini Ufaransa, PSG. Mchezo mwingine ambao utapigwa leo ni pamoja na Ajax ambao watakuwa kwenye uwanja wa nyumbani na kuwakaribisha Juventus. Japokuwa Juventus walionesha ubora wa hali ya juu katika mchezo wao dhidi ya Atletico Madrid baada ya kuwafunga mabao 3-0, huku mchezo wa kwanza Juventus wakifungwa mabao 2-0, bado Ajax wanaogopwa kutokana na aina ya uchezaji wao. Ajax wamefika hapo baada ya kuwaondoa mabingwa watetezi Real Madrid kwa jumla ya mabao 5-2, huku mchezo wa kwanza Ajax wakiwa nyumbani na kufungwa mabao 2-1, lakini marudiano kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu waliweza kupindua meza kibabe na kushinda mabao 4-1. Kutokana na hali hiyo, Ajax bado wanaonekana kuwa tishio kwa Juventus na wakiwa na lengo la kutaka kulipiza kisasi cha mwaka 1996 kwenye fainali za michuano hiyo, ambapo dakika 90 zilimalizika kwa sare ya 1-1, lakini Ajax wakaja kukubali kichapo cha mabao 4-2 ya mikwaju ya penalti. Habari njema kwa Juventus ni uwepo wa mshambuliaji wao, Cristiano Ronaldo ambaye alikuwa anasumbuliwa na majeraha ya nyama za paja, lakini hata kama atacheza mchezo huo, basi anaweza asiwe fiti kwa kiasi kikubwa.
4
Serikali ya Tanzania imesema imeanza mchakato wa kuhakikisha shughuli za utalii zinarejea kama kawaida licha ya ugonjwa wa corona unaondelea nchini na katika mataifa mengine. Mpango huo umebainishwa na Waziri mali asili na utalii Dk Khamisi Kingwangala ambaye jana alisema kutokana na mlipuko wa virusi vya corona kuna hatari ya kupotea kwa ajira takrinani laki 5 za sekta ya utalii huku Matrilioni ya Shilingi yakipotea. Dk Kingwangalla amesema utaratibu mahususi wa kuwalinda wageni wanaofikia nchini na kuchukua tahadhari zote muhimu, “Hakuna haja ya kuzuia wasafiri tena wakati ugonjwa ushaingia”. Kwa kuwa ugonjwa umeishaingia nchini, na kwenye jamii, hai-make sense kuweka masharti magumu kwa watu kuja Tanzania. Tunadhani mkakati wa ‘mandatory quarantine at own cost’ ya siku 14 uondolewe na tuimarishe ‘mandatory mask’ kwa kila mtu, social distancing and hygiene practices. pic.twitter.com/aqcpRRqgeX — Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) May 8, 2020 Tumeanza kujipanga ndani ya Wizara ili kushawishi serikali yote kukubali namna ya kufungua biashara ya utalii mwezi Juni 2020. Tumefanya utafiti na tathmini (scenario analysis), kuna hatari ya ajira 477,000 kupotea kutokana na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na nchi mbalimbali pic.twitter.com/m2n98PEHEq — Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) May 8, 2020 Tutaweka mikakati ya kuhakikisha usalama wa watalii na wafanyakazi kwenye mnyororo wa utalii kuanzia aiport mpaka room ya mgeni. Tutaweka protocol ya usalama na usafi, Pia utaratibu wa namna ya kukagua kampuni na facilities zake kama zimekidhi viwango vya usalama tutakavyoweka. pic.twitter.com/vYDwLKWJ71 — Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) May 8, 2020 Tutatoa COVID-19 safety clearance kwa kampuni za utalii kabla ya kuziruhusu zipokee watalii. Hivyo zitakazofanya biashara zitakuwa tu ni zile ‘COVID-19 Safety Certified Companies’, status ambayo tutaitoa kwa kampuni husika baada ya kukagua facilities zake! pic.twitter.com/JCaMH2M7MW — Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) May 8, 2020
5
Wametoa kilio chao wakati wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti walipotembelewa katika mashamba yao, ambako waliangua kilio kutokana na kutumia fedha nyingi katika uzalishaji, lakini sasa wakibaki njiapanda kutokana na kutojua pa kuuzia tumbaku yao.Mwenyekiti wa Kaliua Farmers Associations, Morris Rubundi alisema licha ya serikali kuivunja TTB na kuvunja uongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku (WETCU), lakini mpaka sasa hawana mwelekeo wa mahali pa kuuzia tumbaku hiyo.Alisema muungano wao wa wakulima wa kujitegemea (IF) na vyama walipewa makadirio ya kuzalisha kilo milioni 3.7, lakini wakati wakiendelea na uzalishaji, walipokea barua ya kufutwa katika uzalishaji wa tumbaku.Alisema wakulima wa kujitegemea mkoani Tabora wanazalisha tumbaku bila kutegemea mkopo wa pembejeo, kwani wao wana uwezo wa kutumia thamani ya mali zao kukopa benki yoyote nchini kuanzia Sh milioni 100.Katibu Mkuu wa Kaliua Farmers Associations, Thomas Kimogwa alisema hadi kufikia sasa ambapo tayari wanakaribia kufungua msimu wa mauzo, hawajapokea vifungashio kutoka kampuni za ununuzi hali inayowatia wasiwasi wa jinsi ya kuuza tumbaku waliyoizalisha.Alisema kumekuwepo na tuhuma nyingi kutoka Wetcu kuwa wao sio wazalishaji, bali ni walanguzi wa tumbaku, jambo ambalo halina ukweli wowote kwa kuwa lengo la Wetcu ni kuwadidimiza wakulima kwa kujali maslahi yao binafsi.Mmoja wa wakulima wa kujitegemea na mdau mkubwa wa zao la tumbaku, Juma Mlewa alisema vyama vya ushirika haviwezi kumsaidia mkulima katika kujikwamua kiuchumi kutokana na kuwa chini ya dalali wa kampuni na taasisi cha kifedha.Alisema kwa muda mrefu wakulima wa tumbaku wamekuwa masikini kutokana na kulipa madeni ya mikopo ya benki yasiyoisha huku Wetcu wakizidi kujikusanyia mabilioni ya fedha kutoka kwa wakulima hao na kuwaacha katika dimbi la umasikini.Alisema ili kufikia malengo ya kila mkulima kunufaika na kilimo cha tumbaku, kuna haja ya serikali kufuta utitiri wa vyama vya ushirika na kubaki vyama vyenye uwezo wa uazilishaji kama walivyo IF na Associations.Aidha, aliomba serikali kuunda bodi isiyokuwa na mlengo wa kisiasa na ambayo haitaegemea upande wa wowote wa kutaka kuwanyonya wakulima wa tumbaku kama bodi iliyokuwepo hivi sasa ilijali kujipatia fedha kwa kuwanyima haki walengwa wa zao hilo.
5
KOCHA wa Yanga, Luc Eymael amefagilia matokeo ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Eymael alisema matokeo hayo yamewapa nguvu mpya ya kushindania taji la Ligi Kuu linaloshikiliwa na wapinzani wao Simba.Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulifanyika juzi kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam ulishuhudia Yanga ikipata bao hilo pekee la ushindi kipindi cha pili kupitia kwa mchezaji David Molinga akimalizia pasi ya Ditram Nchimbi.Eymael alisema matokeo ya kushinda bila kuruhusu kufungwa ni mara ya pili inatokea kwa kikosi hicho wakianza dhidi ya Tanzania Prisons kwenye kombe la Shirikisho la Azam (FA) kwa mabao 2-0 hivyo hayo ni maendeleo mazuri kwa timu kutafuta ushindi mechi inayokuja dhidi Lipuli FC.“Kupata ‘Clean Sheet’ ni matokeo mazuri kwangu kama kocha lakini pia mchezo ulikuwa mgumu na tumepata matokeo yanayozidi kutupa nguvu na wachezaji na kuendelea kupambana kupigania nafasi ya ubingwa wa ligi,”alisema Eymael.Alisema mchezo huo dhidi ya Mtibwa ulikuwa mgumu kutokana na muda mwingi wapinzani wao walikuwa wanacheza kwa kujilinda na kutumia nguvu kubwa hali iliyowafanya kubadili mbinu na kutumia pasi ndefu zilizowanufaisha.“Siku zote nimekuwa nikiwaambia wachezaji wangu wasipende kucheza mchezo wa nguvu na kukamia kwa sababu lolote linaweza kutokea ndiyo maana kwenye mchezo wa leo (juzi ) wapinzani wetu walikuwa wanacheza mfumo huo na hasa walikuwa wanamfanyia Benard Morrison ambaye baadae nilimfanyia mabadiliko,” alisema Eymael.Naye Kocha wa Mtibwa, Zuberi Katwila alisema amekubali matokeo hayo na kudai wanajipanga kwa kusahihisha makosa waliyoyafanya kupoteza mchezo huo kujipanga na mechi ijayo dhidi ya Ruvu Shooting.“Wachezaji wangu walicheza vizuri na walijitahidi kufuata maelekezo na tulifanya kosa moja ambalo wenzetu walitumia kupata ushindi kikubwa tunaenada kujipanga kwa mechi inayokuja kutafuta matokeo kwa kuwa hii ni ligi lolote linaweza kutokea,” alisema Katwila.
4
TPB ili kufungua tawi lake jipya wilayani humo jana ili kusogeza karibu huduma za kifedha kwa wananchi.Akizindua tawi hilo, Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru alisema uanzishwaji huo ni hatua ya kimaendeleo na itasaidia kuwavutia wawekezaji katika soko la hisa na kuwashawishi wateja wadogo kuwekeza kutokana na benki hiyo kukuza amana na biashara zake.Mafuru aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, alisema ukuaji wa amana na biashara wa benki hiyo kwa miaka minne kutoka Sh bilioni saba hadi Sh bilioni 40, umewezesha benki hiyo kuwa na mabadiliko ya soko na uchumi.Alisema hatua hiyo pia imeiwezesha benki hiyo kubaki na azma yake ya kutimiza dhamira ya kupeleka huduma za kibenki karibu zaidi na wateja, hasa wateja wadogo tangu ilipoanzishwa kwake 1925.Mafuru alisema baadhi ya taasisi za umma za kibenki, zimeshindwa kujiendesha vizuri na nyingine kufa kutokana na kupoteza fedha kila mwaka na kupata hasara, kwa kuwa zililenga kuwahudumia wateja wakubwa zaidi na kukosa usimamizi mzuri wa mikopo.“Hali hii imebadilika kwa Benki ya Posta imeweza kuwa na ukuaji wa faida kutoka 2010 licha ya serikali kuwekeza mtaji mdogo, nawapongeza sana na nataka mashirika mengine yaige mfano huu wa kutumia elimu ya kuwahamasisha wateja wadogo ambao ndio wengi hasa wa vijijini,” alisema Mafuru.Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB, Profesa Lettice Rutashobya alisema katika jitihada za kuwafikia watanzania katika makundi yoyote ili kupata huduma za kibenki, benki hiyo imeanzisha akaunti maalumu kwa ajili ya vikundi ili viweze kujiwekea akiba benki na kupata mikopo.Alisema sehemu kubwa vikundi, vimeshindwa kupata huduma za kibenki kwa sababu mbalimbali kama kutokuwa na elimu ya uhamasishwaji wa kujiwekea akiba, kutokubaliwa kufungua akaunti kwa ugumu wa vielelezo vinavyotakiwa na umbali mrefu kufikia huduma za kibenki.Rutashobya alisema kufunguliwa kwa tawi la Babati la benki hiyo, kutasogeza huduma kwa wastaafu katika kupata mikopo na huduma za kibenki kwa wananchi wengi waishio pembezoni mwa wilaya hiyo. Aliwataka wakazi wa Babati, kuchangamkia fursa zinazotolewa na benki hiyo.Alisema kuwa kutokana na ongezeko la watu, tawi la awali halikutosheleza mahitaji ya wakazi wa mji na vitongoji vyake kutokana na udogo wake. Alisema bodi iliamua jengo jingine lijengwe, lililogharimu Sh milioni 600 kutimiza azma ya kupeleka huduma karibu na wateja wake.Kabla ya uzinduzi wa tawi hilo, benki hiyo ilitoa msaada wa magodoro 20 na mashuka 40 ya thamani ya Sh milioni nne kwa Kituo cha Afya cha Magugu wilayani Babati ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya.Akikabidhi msaada huo, Profesa Rutashobya alisema utapunguza adha ya wagonjwa kulala chini kipindi cha kupata huduma za afya na kwamba benki hiyo ni sehemu ya jamii na inawajibika kwa hilo.Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Dk Christian Kahembe, alishukuru msaada huo na kusema kituo hicho kina uhaba wa majengo, wodi za kulaza wagonjwa na dawa. Alisema kwamba msaada uliotolewa, utawasaidia wagonjwa wengi wakiwamo wajawazito na watoto na hatimaye kupunguza vifo vya watu hao.
5
OSCAR ASSENGA, TANGA Wizara ya Nishati imesisitiza kwamba mradi wa bomba la mafuta kutoka hoima nchini Uganda hadi Tanzania eneo la Chongoleani mkoani Tanga bado upo na unaendelea kutekelezwa baada ya tofauti ya Uganda na wawekezaji. Kauli hiyo imetolewa leo na Mratibu wa Mradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Wizara ya Nishati, Salum Mnuna wakati wa kikao cha kutoa mrejesho kwa watendaji wa mkoa, wilaya na serikali za vijiji kuhusu mradi huo. Amesema kuwa tofauti ya Uganda na wawekezaji ilitokea katika manunuzi ya hisa za moja ya waombaji wa kampuni ya dalo kukamilishwa huku akieleza kwamba kuna kazi zimesimama lakini kazi za msingi zimekamilishwa ikiwemo usanifu wa mradi, utambuzi wa njia. Awali akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella alisema kwamba mradi unaelekea kwenye hatua ya kutwaliwa ardhi pamoja na hatua hiyo kufikiwa lakini kumekuwa na changamoto kwa wenzao wa Uganda. Alisema changamoto hizo ni za kawaida kwenye miradi mikubwa hivyo serikali imewahakikishia zitashughulikiwa ikiwezekana mwakani shughuli zote za msingi ziwe zimekamilika na ujenzi uanze. “Ndugu zangu washiriki kwenye mkutano huu tuende kuwafikishia ujumbe huu wananchi ambao mradi utapita waendelee kuwa na subira mradi unakuja wajiande kunufaika na fursa za bomba”. “Lakini nisisitize kwamba fursa za ajira na nyengine bado hazijaanza rasmi kwa sababu utekelezaji wake upo hatua ya mwanzo, pasipatikane watu ambao wanatangaza fursa za ajiraza bomba la mafuta,” amesema Shigella.
3
LICHA ya Tanzania kupata mwaka 1961, wananchi wa Kata ya Lufu, wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma, wamedai kwamba haukuwanufaisha, lakini uhuru uliowafaidisha ni wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (Tarura) kuwajengea barabara ya kufi ka katika kata hiyo.Wakizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa Dodoma, Dk Binilith Mahenge ambaye ni mkuu wa mkoa wa kwanza kufika kwenye kata hiyo tangu kuanzishwa kwake miaka 22 iliyopita, wamedai kwamba uhuru wao ni baada ya barabara hiyo kujengwa. Kata hiyo iliyopo kwenye vilele vya milima takribani mita 3,000 kutoka usawa wa bahari, ilikuwa haifikiki hadi ilipochongwa mipangano ya milima urefu wa kilomita 17 kufika kwenye kata hiyo.Mkazi wa Lufu, Stephan Mtambulo alisema tangu kuanza kwa kata hiyo mwaka 1997 haikuwa na barabara ya kufika hapo, lakini mwaka huu Tarura imewajengea barabara na vijiji vya kata hiyo vinafikika. Mtambulo alimpongeza Mkuu wa Mkoa, Dk Mahenge kwa kuwa mkuu wa mkoa wa kwanza kufika katika kata hiyo tangu miaka 22 iliyopita, akasema wao wanaamini kwamba ukombozi wa kweli na ujio wa kiongozi huyo unatokana na uwepo wa barabara hiyo.Alisema kabla ya Tarura kuchimba miamba na kuchonga miinuko na kujenga barabara hiyo, walikuwa wapo kisiwani, kwani walipata taabu katika kusafirisha wagonjwa kwenda hospitalini na mazao kwenda sokoni. “Wakati mwingine tulitumia punda na wakikosekana tulibeba wagonjwa kwenye machela na mazao tulibeba kichwani na kutembea umbali wa kilometa 17 kufikisha barabarani,” alisema.Alisema wajawazito walipata taabu wakati mwingine walijifungulia njiani, wengine walipoteza maisha kabla ya kufika katika Hospitali ya Wilaya Mpwapwa iliyopo umbali wa kilometa 101 kutoka kijijini hapo. Erasto Ndiuka alisema mazao yao mengi yanayostawi katika uwanda huo wa juu yakiwamo mahindi, mtama, uwele, viazi na viazi viatu, walishindwa kuyafikisha sokoni Kibakwe na Mpwapwa Mjini, hivyo yaliozea shambani. Jonathan Kidenyike alisema licha ya kukosa miundombinu ya barabara, kata hiyo pia haina sekondari, hivyo wanafunzi wao wakifaulu wanatakiwa kwenda kusoma sekondari ya kata jirani ya Luwundwa umbali wa zaidi ya kilomita 10 na wengi waliacha masomo.“Kutokana na sekondari kuwa mbali, wanafunzi wengi kutoka shule za msingi Ilala, Mlimo na Gomuhungilo waliofaulu kuendelea na masomo ya sekondari, wasichana walipata ujauzito kutokana na kupanga nyumba kijijini huko na wavulana waliacha na kuingia kwenye shughuli nyingine,” alisema. Jurica Makuya alisema barabara hiyo ndiyo uhuru wao, kwani sasa wanaweza kusafirisha wagonjwa wao na kurudisha maiti kwa gari kutoka hospitali, tofauti na zamani ambapo walihitaji kubeba mzega au machela mabegani.Mkuu wa Mkoa, Dk Mahenge aliwashukuru wananchi hao kuipongeza serikali ya awamu ya tano kwa ujenzi wa barabara hiyo. Kuhusu mazao yao kukosa soko, Dk Mahenge alimwagiza Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo, Paulo Sweya kuweka mkakati wa kuangalia ni namna gani wanaweza kuwa na gulio la kuuza mazao yao.Sweya alisema halmashauri hiyo imejipanga kusaidia ujenzi wa shule hiyo mara wananchi wa kata hiyo watakapoandaa eneo la kujenga shule na wawe tayari kuchangia nguvu zao katika hatua za awali hadi kwenye rinta. Barabara wanayoita imeleta uhuru katika kijiji na kata ya Lufu iliyopo juu ya milima zaidi ya mita 3,000 kutoka usawa wa bahari ilikuwa haipitiki kwa muda mrefu sasa inafikika baada ya Tarura kuchonga milima umbali wa km 17 hadi katani hapo.
3
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja Mwendeshaji wa kampuni hiyo, Baraka Shelukindo alisema, kuanzia sasa visimbuzi vya DStv vitauzwa Sh 79,000, ikiwa ni pamoja na kupata kifurushi cha mwezi cha DStv Bomba.Alisema katika msimu huu wa kuelekea kwenye sikukuu za mwisho wa mwaka, kampuni hiyo imeona vema kuwazawadia Watanzania kwa kutoa ofa hiyo pamoja na kuzindua kifurushi cha kitanzania cha DStv Bomba, kinachouzwa Sh 23,500 kwa mwezi.Akizungumzia kifurushi hicho ambacho Balozi wake ni mwanamuziki wa kizazi kipya nchini, Nassib Abdul (Diamond Platnumz), Shelukindo alisema kina zaidi cha chaneli 65 za vitu tofauti ikiwemo makala, michezo, habari na tamthilia.Kwa upande wake, Diamond alisema kifurushi hicho kimekuja kwa wakati kwani watanzania wengi wanapenda kupata chaneli zinazokidhi matakwa yao na kwamba hata bei yake ni nafuu ikilinganishwa na ubora na wingi wa chaneli katika kifurushi hicho. “Ni kifurushi kizuri chenye chaneli zilizo jaa maudhui ya jamii yetu ya Tanzania.
5
AKIANDAMWA na wakosoaji kwa kuteua au kufikiria kuteua watu wenye sifa mbaya ikiwamo ukiukaji wa haki za binadamu katika nyadhifa mbalimbali za utawala wake, Rais mteule Donald Trump sasa anaonywa juu ya uwezekano wa kutodumu madarakani. Ni kutokana na kuonesha nyendo zinazotia shaka za mgongano wa maslahi katika kipindi hiki cha mpito, akijiandaa kuingia Ikulu ya Marekani, White House. Kipindi cha wiki mbili tangu ashinde uchaguzi wa Novemba 8, ahadi yake ya kutenganisha biashara zake na maisha yake ya urais imezua maswali. Amekuwa akikutana na wafanyabiashara na wanasiasa katika hoteli yake kubwa ambayo haiko mbali na White House na kuwatia wasiwasi wakosoaji iwapo kweli ataweza kutenganisha biashara zake na Ikulu. Simu za Kamati ya Bunge ya Uchunguzi ziliripotiwa kukumbwa na msongamano wa miito ya simu Ijumaa iliyopita kufuatia mitandao ya jamii kuitaka kamati hiyo imchunguze Trump kwa kile wanachoona mgongano wa maslahi. Wiki hii Trump alikutana na wafanyabiashara wa India ambao ana ushirika nao, Atul Chordia, Sagar Chordia na Kalpesh Mehta, wanaojenga pia jengo la kifahari la Trump mjini Mumbai. Wakati Msemaji wa Trump Organization akiliambia gazeti la New York Times kuwa  mkutano huo haukuwa rasmi, vibopa hao wa India walitumia fursa hiyo kukutana na watoto wa Trump. Watoto hao wanachukua uendeshaji wa biashara zake, wakati huo huo wakibakia katika timu ya mpito ya baba yao huyo wakionekana kuwa na ushawishi katika teuzi mbalimbali. Mehta aliliambia gazeti la Economic Times kuwa Donald Trump Jr. ameeleza kuridhishwa na biashara za kampuni nchini India na ameonesha nia ya kupanua zaidi biashara nchini humo. Akizungumza baada ya ushindi wa Trump, aliliambia gazeti hilo la uchumi: “India ina idadi kubwa ya miradi ya Trump hasa mali zisizohamishika, ikiwa kubwa zaidi nje ya Amerika ya Kaskazini. Trump ana mikataba inayoendelea mitano nchini humo yenye thamani ya dola bilioni 1.5. “Uzalishaji umeanza katika miradi miwili na miradi mitatu zaidi inatarajia kuzinduliwa mwaka 2017 na tunaendelea kusaka fursa zaidi,” alisema. Miradi ya Trump nchini  India ni miongoni mwa biashara alizonazo ng’ambo ikiwamo nchini Uturuki, Indonesia, Israel, Dubai, Panama na  Philippines. Nyota huyo wa zamani wa televisheni pia anadaiwa mkopo wa dola milioni 364 na pia anadaiwa na Benki ya China na Goldman Sachs. Aidha ameonana na mabalozi kutoka nchi za Kiarabu katika hoteli yake ya nyota tano mjini Washington na kuzua utata mkubwa kwa vile wanadiplomasia hao wameripotiwa kulala katika hoteli hiyo mpya. Wakati akionana na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe mwishoni mwa wiki, katika tukio lingine lililozua utata ilhali Rais Barack Obama bado yu madarakani, binti yake Ivanka alikuwapo katika mkutano huo sambamba na mumewe Jared Kushner. Si Ivanka wala Kushner ambao wana kibali kinachowaruhusu kuwapo katika mkutano kama huo. Baadhi ya wanasheria wanaonya Trump anaweza kushitakiwa bungeni na hata kuvuliwa urais atakapoapishwa kwa kitendo hicho. Barua pepe iliyotumwa na kampuni yake Ivanka inayojishughulisha na vito vya thamani kufuatia kuonekana kwake katika kipindi cha luninga cha “60 Minutes” akiwa na baba yake pia ilikuja kama mshangao. Iliwafahamisha wateja wapi wanaweza kununua bangili zenye thamani ya dola 10,800 sawa na Sh milioni 22 alizokuwa amevaa Ivanka siku hiyo. Trump amesema atawaachia wanae waendeshe himaya yake ya kibiashara katika mfuko ujulikanao kama “Blind Trust.” Lakini kinadharia, blind trust ambao huhusisha kuuza mali na kuzibadili kwa kuzifanya ziwe tofauti na zile Trump anazozijua , kwa mfumo wa sasa kuwatumia wanawe ni kitu kisichowezekana. Kushner ameripotiwa kutafuta ushauri iwapo anaweza kuingia katika utawala wa Trump, huku timu ya mpito ya Rais Mteule ikijaribu kupata kibali kwa ajili ya mkwewe huyo, ambaye pia ni mfanyabiashara wa majengo na mmiliki wa gazeti la New York Observer. Sheria inayokataza upendeleo wa kindugu ilipitishwa mwaka 1967 miaka michache baada ya Rais John F. Kennedy kumfanya kaka yake Robert, kuwa mwanasheria mkuu. Kwa mujibu wa sheria hiyo, Rais hawezi kumteua mwanandugu kuingia katika shirika wakala au wadhifa wowote serikalini. Ushawishi wa Kushner tayari umeelezwa kufanya yake. Ni baada ya Gavana wa New Jersey, Chris Christie kuondolewa kwa mshangao wa wengi kutoka uenyekiti wa timu ya mpito sambamba na wasaidizi wake wengine licha ya kazi nzuri waliyofanya wakati wa kampeni. Inasemekana chanzo ni ushawishi wa huyu Kushner, uhasama ukianzia mapema miaka ya 2000 wakati baba yake Kushner, bilionea wa majengo Charles Kushner, ambaye pia alikuwa mfadhili maarufu wa chama cha  Democratic aliposhitakiwa kwa mashitaka ya ukwepaji kodi na kujaribu kuharibu ushahidi. Kesi hiyo ilikuwa chini ya Christie, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa New Jersey, ambaye alijipatia umaarufu mkubwa kwa kuisimamia vyema huku vyombo vya habari vikitengeneza vichwa vya habari zilizouza mno. Katika kesi hiyo, Charles alihukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka miwili jela. Miaka zaidi ya kumi baadaye imemkuta Christie akiwa ndani ya timu moja na mtoto wa bilionea huyo, lakini habari mbaya sana kwake ni mkwe wa bosi wake. Kwamba kijana Jared Kushner (35), mtoto wa bilionea Charles, ni mume wa Ivanka Trump na zaidi ya hilo ni mshauri mwenye nguvu na ushawishi na anayeaminiwa zaidi kuliko wote na Trump. Minong’ono iwapo wanafamilia wa Trump wataendelea kuwapo White House, inabakia kutokuwa rasmi lakini wanaweza kuikwepa sheria hiyo ya upendeleo kwa kitu kama Kushner kuwa mshauri wa bila malipo. Makamu wa Rais Mteule Mike Pence tayari amejaribu kuzima wasiwasi unaozingira mgongano wa maslahi wakati akihojiwa hivi karibuni na Fox News. Ni kuhusu iwapo watoto wa Trump kuendesha biashara kunaweza kutengeneza mgongamo hatari wa maslahi. Gavana huyo wa Indiana alisema kuwa ana imani Trump atajikita katika masuala ya wananchi na kuhakikisha kuna utengano mzuri wa biashara zake na siasa. Hata hivyo, hilo ni suala la kusubiri na kuona.  
2
MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi (pichani) amesema halmashauri yake imetenga Sh bilioni 1.2 kwa ajili ya kutoa mikopo nafuu kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.Kunambi alibainisha hayo jijini hapa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kumaliza ziara ya kuangalia utekelezaji wa miradi ya kuboresha jiji la Dodoma.Kunambi alisema Halmashauri ya Jiji la Dodoma ndio halmashauri pekee iliyotenga fedha nyingi kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza sheria ya kutoa mikopo kwa vijana, watu wenye ulemavu na wanawake.Sheria inazitaka kila halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kila mwaka ambazo wanatakiwa kuzitoa kama mkopo kwa makundi ya vijana na wanawake ambapo kila kundi litapewa asilimia nne ya mapato na watu wenye ulemavu asilimia 2.Kunambi alitumia fursa hiyo kuhimiza wahusika wa makundi hayo kuchangamkia fursa hiyo ya kupata mikopo ili waweze kuendesha shughuli halali zitakazowaongezea kipato chao. “ Halmashauri ya jiji ndio pekee inayotenga fedha nyingi kwa ajili ya mikopo nafuu sana ka vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, hivyo niwahamasishe wale walio katika makundi haya kuchangamkia fursa. “Unachoweza kufanya ni kuunda kundi na mje ofisini mkiwa na andiko la mradi ambalo litaonyesha shughuli mnayotaka kufanya na jinsi mtakavyourejesha mkopo,” alisema.Katika hatua nyingine, Kunambi amewataka vijana kuchangamikia fursa za ajira zilizojitokeza kwenye mradi wa ujenzi wa mji wa kisasa wa Serikali na miradi mbalimbali ya ujenzi inayoendelea jijini. “Ninawaomba ndugu zagu vijana wa hapa ,mjitokeze kuchangamkia fursa hizi ili kujiongezea kipato mkichelewa watajitokeza wengi kutoka mbali kuja kuomba ajira maeneo hayo”alisema Kunambi.Aliyataja makundi mengine yanayoweza kunufaika na mradi huo wa ujenzi ni akinamama lishe kwani kuna kundi kubwa la mafundi wanaotekeleza ujenzi huo wanahitaji chakula, wajasiriamali wa kuponda kokoto wanaweza kujitokeza kuuza kokoto kwani inahitajika kwenye eneo hilo la ujenzi.Kunambi alisema Jiji hilo litakuwa na miradi mingi mballimbali ya ujenzi ikiwa pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa unaoendelea kutoka Dar es salaam hadi Makutupora kwa awamu ya kwanza na ile ya miundo mbinu ya barabara. “Hadi kukamilika kwa miradi hiyo wananchi watafanikiwa na kunufaika kiuchumi hivyo wachangamkie fursa hizo za ajira,” alisema. Hivi karibuni akiwa kwenye ukaguzi wa ujenzi wa ofisi za wizara 24 katika Mji wa Serikali, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Kunambi kushirikiana na mwenzake wa Chamwino kuhakikisha vijana wengi wanapata fursa za ajira kwenye mradi huo.Majaliwa alisema: “Mkurugenzi wa Jiji wasiliana na Mkurugenzi mwenzako wa Chamwino mhakikishe vijana na akina mama wanakuja kufanya kazi hapa. Pia itisha kikao cha waandishi wa habari uwaeleze wananchi wako fursa zilizopo, kuanzia ufyatuaji wa matofali, uuzaji wa nondo, kokoto na utengenezaji wa pavement blocks, hizi zote ni fursa, tuna wizara 24 na mahitaji ni makubwa.”
3
WAKATI Rais John Magufuli akitoa miezi minane kwa mkandarasi wa daraja la Mto Sibiti kukamilisha, tayari ujenzi huo umefikia asilimia 90 na huenda ukakamilika kabla ya muda uliopangwa.Septemba 10, mwaka huu, Rais Magufuli akiweka jiwe la msingi la daraja la Mto Sibiti ambalo ni kiunganishi cha mikoa ya Simiyu na Singida kupitia wilaya za Meatu na Mkalama, alimuagiza mkandarasi kupitia Kampuni ya Hainan kufanya kazi hiyo usiku na mchana na ndani ya miezi nane liwe limekamilika.Baada ya agizo hilo, gazeti hili limetembelea kukagua ujenzi wa daraja hilo na kushuhudia tayari wananchi wakipita juu ya daraja hilo kwenda katika shughuli zao za kiuchumi kwa kutumia ngazi huku ukamilishaji ukiendelea badala ya kutumia mitumbwi kama awali.Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wamemshukuru Rais Magufuli kwa kuhakikisha ujenzi wa daraja hilo unakamilika kwa wakati na kuwaondolea adha ya muda mrefu ya kuvuka mto huo kwa mitumbi na wakati mwingine kusababisha maafa ya watu na mifugo mingi kusombwa na maji. “Tulikuwa tukipata shida sana hapa, wakati wa vipindi vya mvua hasa masika wananchi tulikuwa tunavuka kwa shida sana na kama unavyouona huu mto ulivyo jaa leo ingekuwa shida kama daraja hili lisingekuwepo, na tuna kila sababu ya kumshukuru Rais Magufuli,’’ alisema mkazi wa Kijiji cha Bukindi Meatu, Felister Mohamed.Ujenzi wa daraja hilo umekuwa ni mkombozi kwa watu wengi wakiwepo wafugaji na wakulima ambapo baadhi ya wafugaji wamesema sasa usalama wa mifugo yao na mazao utakuwa ni wa uhakika tofauti na hapo awali. Mfugaji Kurwa Mgembwa alisema kukamilika kwa daraja hilo hadi hapo lilipofikia kwao ni ukombozi kwani wameanza hata kuvusha mifugo kwa kutumia ngazi jambo ambalo wanaona kwao kama msaada mkubwa. Aidha, baadhi ya wananchi kutoka vijiji vya Mkalama walisema kukamilika kwa ujenzi huo wa daraja ni ufunguzi rasmi wa mlango wa uchumi kwao kwani sasa wana uhakika wa kufanya biashara baina ya wilaya mbili zinazounganishwa na daraja hilo za Meatu na Mkalama.“Tangu nchi hii ipate uhuru ndio sasa daraja hili limejengwa, wananchi wa Mkalama tutafaidika sana maana tulikuwa tukipata shida hata ya kufika katika mnada uliopo hapa jirani katika kijiji cha Bukundi maana unaweza ukaenda na mvua kubwa ikinyesha ikakukuta huko, uwezo wa kurudi nyumbani haupo tena,” alisema mkazi wa Mkalama, Kayanda Ndaki.Mkurugenzi wa Kampuni ya Kimataifa ya Hainan, He Zhen alisema kazi ya ujenzi huo imefikia asilimia 90 na mapema Februari mwakani magari yote yataanza kupita juu daraja hilo. Alisema changamoto kubwa wanayopambana nayo sasa hivi ni suala la mvua sambamba na wizi wa vifaa vya ujenzi pamoja na mafuta ya magari ambao unafanywa na wafanyakazi wa kampuni hiyo wasio waaminifu kwa kushirikiana na wananchi wa vijiji vya wilaya za Meatu na Mkalama.
3
NA WINFRIDA MTOI MWANARIADHA Augustino Sulle, amefanikiwa kuvunja rekodi ya taifa ya marathon, iliyokuwa inashikiliwa na mkongwe, Juma Ikangaa, baada ya juzi kukimbia akitumia saa 2:7:44 katika  mbio za Toronto Marathon, nchini Canada. Sulle alivunja rekodi hiyo ya kukimbia kilomita 42, akimpiku Ikangaa ambaye mwaka 1989 alikimbia  mbio za marathon zilizofanyika nchini Marekani akitumia saa 2:8:1. Katika mbio hizo za Toronto, Mkenya, Benson Kipruto, aliibuka kidedea akiwa mshindi baada ya kutumia saa 2:07:24, nafasi ya pili akishika Sulle, wakati nafasi ya tatu ilichukuliwa na Felix Kandie, pia wa Kenya, aliyetumia saa 2:08:30. Akizungumza na MTANZANIA jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday, alisema ushindi huo ni mkubwa kitaifa licha ya kushika nafasi ya pili katika michuano hiyo ya Canada. Gidabuday alisema kuanzia sasa Sulle anakuwa mwanariadha mwenye rekodi kubwa nchini hadi pale atakapotokea mwingine na kumpiku. Alisema mwanariadha huyo anahitaji pongezi kwa sababu mashindano hayo ni makubwa, yanatambulika na Shirikisho la Kimataifa la Riadha (IAAF). “Sulle anastahili sifa, amefanikiwa kushika nafasi ya pili katika mashindano makubwa na kuweka rekodi mpya kitaifa kwa kuwa mara ya mwisho ilipatikana miaka 29 iliyopita kupitia Juma Ikangaa, hivyo anastahili sifa,” alisema  Gidabuday. Alifafunua kuwa ushindi huo umepokelewa kwa furaha na shirikisho la mchezo huo, pia inawapa nguvu ya kuendelea kutengeneza wanariadha bora  ili kuja kuvunja rekodi katika mashindano mbalimbali. Alisema mwanariadha huyo anatarajia kuwasili nchini kesho, pia wanariadha wengine waliokuwa katika mashindano yaliyofanyika Japan juzi nao watawasili siku hiyo. “Wapo wanariadha wengine wamepata medali nchini Japan, lakini mashindano yao hayakuwa makubwa na hayatambuliki na shirikisho la kimataifa kama ilivyokuwa kwa Sulle,” alisema.
4
VINARA wa kikundi cha kihalifu kinachojulikana kwa jina na Tatu Mzuka kinachofanya vitendo vya kihalifu jijini Arusha wametiwa mbaroni na Polisi mkoani humo. Aidha watuhumiwa wamekiri kuhusika katika matukio mbalimbali ikiwamo uporaji, unyang’anyi wa vitu vyenye thamani na wizi huku walengwa zaidi wakiwa wanawake. Mbali ya vinara hao, wengine 11 wamekamatwa wakipata maelekezo ya kufanya uhalifu kutoka kwa vinara hao nao wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakama kujibu mashitaka yao. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Jonathan Shana aliwataja vinara watatu kati ya 13 ambao wakuwa wakiongoza kundi hilo kuwa ni Faisal Mbaraka (19), Emmanuel Bosco (18) na Mohamed Hussein (18) wote wakazi wa Sanawari jijini Arusha.Alisema kukamatwa kwa kundi hilo ni kutokana na operesheni iliyofanywa na jeshi hilo kwa siku tatu mfululizo katika maeneo mbalimbali jijini hapa. Kamanda Shana alisema katika msako huo wamekamata pikipiki nne; MC 504AHT aina ya Kinglion, MC262AXQ aina ya Boxer, MC240AEB aina ya Boxer na MC 811BWG aina ya Haojue.Vitu vingine ni laptop tatu, televisheni kubwa tatu, meza mbili za televisheni, jokofu moja aina ya Boss na redio kubwa moja ikiwa na spika zake mbili aina ya Sony . Kamanda wa Polisi amewataka wananchi walioibiwa vitu vyao kufika kituoni hapo na kuvitambua. Aidha, alisema katika operesheni hiyo, pia walikamata dawa za kulevya ikiwamo misokoto 524 ya bangi, mirungi bunda 16, bangi kilo 12 na kete mbili za heroine, na dawa hizo zimekuwa zikiuzwa dukani kwa wafanyabiashara
3
BERN, USWISI ZIKIWA zimebaki hatua tano kumalizika kwa michuano ya Tour de France, nyota wa michuano hiyo ya baiskeli, Fabian Cancellara, ametangaza kujitoa akidai kuwa anataka kujiandaa na michuano ya Olimpiki. Hii ni siku ya pili mfululizo kwa nyota wa mchezo huo wa baiskeli kujitoa wakidai kuwa wanakwenda kujiandaa na michuano ya Olimpiki ambayo inatarajiwa kufanyika mwezi ujao nchini Brazil. Jumanne ya wiki hii Mark Cavendish naye alitangaza kuachana na michuano hiyo na leo hii ni Cancellara, ambaye ameachana na michuano hiyo na kukimbilia kwenye Olimpiki. Cancellara, mwenye umri wa miaka 35, raia wa nchini Uswisi, ambaye aliwahi kushinda tuzo ya dhahabu mwaka 2008, amedai kuwa huu ni wakati wake wa kujiandaa na Olimpiki. “Haya si maamuzi rahisi kuyatoa, lakini najisikia kuwa ninafanya jambo sahihi kwa muda huu, najua kuwa timu yangu inashika nafasi ya pili katika michuano hii ya Tour de France, lakini ni bora niachane nayo. “Najua nitaiacha timu yangu katika wakati mgumu, lakini ninawataka mashabiki kuendelea kutoa ushirikiano wao kwa kipindi chote kilichobaki toka sasa. “Ukweli ni kwamba mwili wangu umechoka, hivyo kama nataka kushinda kwenye michuano ya Olimpiki lazima nipate muda wa kupumzika na kama nikisema niendelee na Tour de France nitakosa muda wa kupumzika na sitoweza kufanya vizuri kwenye Olimpiki,” alisema Cancellara. Hii ilikuwa ni hatua ya mwisho kwa nyota huyo kushiriki michuano hiyo mikubwa ya kimataifa, hivyo amewashukuru wote ambao walimpa sapoti. “Katika miaka 12 ambayo nimeshiriki michuano hii, nimejifunza mambo mengi sana, lakini maamuzi haya yananifanya niwe na hisia kali kwa mashabiki wangu kwa kuwa wengi wao walikuwa hawakutegemea jambo kama hili. “Napenda kuwashukuru viongozi wa mashindano ya Tour de France kwa kipindi cha miaka yote na ubingwa ambao niliuchukua, najua hii ni historia kwangu,” aliongeza.
4
MWANASIASA mkongwe nchini, Paul Kimiti ameeleza kukunwa na maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali ndani ya miaka 58 ya Uhuru, huku akishangazwa na namna Serikali ya Awamu ya Tano ilivyofufua Kampuni ya la Ndege Tanzania (ATCL).Kimiti ambaye amewahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, aliyehudumu miaka miwili na kisha kujiuzulu, amesema hakutegemea shirika hilo kufufuka ndani ya muda mfupi na kufika ilipo sasa.“Sikutegemea kama ndani ya muda mfupi ATCL ingeweza kufikishwa hapo ilipo. Mpaka sasa nashangaa. Mbinu aliyotumia rais huyu (Dk John Magufuli), hata mimi nisingeifikiria hata kidogo. Maana chombo kilidhaniwa kuwa kitafufuka polepole, itaangaliwa misaada kutoka nje. Lakini akaona umuhimu wake akavalia njuga,” alisema.Aliendelea kusema, “Najivunia sana kwa kweli, ilikuwa inanisikitisha kuona ATCL inaanguka hivi hivi. Hakuna msaada tunapata. Nikasema hapa napoteza muda.”Kimiti aliyeteuliwa mwaka 2007 kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, anasema wakati anajiuzulu mwaka 2009, shirika lilikuwa na ndege ndogo zipatazo nne ambazo zilikuwa ni za kukodi. Akizungumza wakati wa mapokezi ya ndege Boeing 787-8 Dreamliner iliyowasili nchini Oktoba mwaka huu, Rais Magufuli alisema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria na imejizatiti kuhakikisha shirika linafufuliwa, kama ilivyo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015.Alisema ndege mpya saba, kati ya 11, zilizonunuliwya na serikali zimewasili. Mbili ni za masafa marefu, mbili ni masafa ya kati aina ya Airbuss 220 na tatu ni za masafa mafupi aina ya Bombadier Dash Q400.Ndege nyingine nne zinatarajiwa kuwasili nchini kwa nyakati tofauti, mojawapo ikiwa ni Bombardier iliyotarajiwa kuwasili nchini hivi karibuni, lakini ikazuiliwa nchini Canada kutokana na kesi iliyofunguliwa na raia wa Afrika Kusini, Hermanus Steyn. Ndege nyingine itawasili Juni 2020 na mbili aina ya Airbus 220 zitawasili kati ya Juni na Julai 2021.Akizungumzia sekta nyingine, mtalaamu huyo wa kilimo alieleza kuridhishwa na serikali inavyoingilia kati mahitaji ya wakulima, hususani bei ikiwamo kuruhusu wauze mazao yao nje ya nchi, akisema inawapa ari ya kulima. Kwa upande wa elimu, pamoja na kupongeza hatua mbalimbali zinazofanywa na serikali ikiwamo utoaji wa elimu bila malipo, Kimiti alishauri mfumo wa elimu uwe ni unaojibu matarajio ya wahitimu kwa maana ya ajira.
3
    Na MWANDISHI WETU, MAISHA ya mwanadamu kwa  sasa yanategemea mno  bidhaa za plastiki katika kuhifadhia  mizigo mbalimbali ikiwamo vyakula, maji na mafuta ya kula. Licha ya kutumika katika matumizi mbalimbali katika kuhifadhia vitu, imebainika kuwa plastiki ina madhara makubwa katika matumizi ya binadamu. Utafiti uliofanywa na Jumuiya ya Madaktari wa Marekani ulitoa tahadhari kuhusu matumizi ya vyombo vya plastiki vinavyotumika kufungashia na kubebea vyakula. Wanasayansi hao wanasema plastiki ina madhara makubwa endapo ikikutana na joto kali na kutoa kemikali iitwayo BPA(bisphenol A). Mwaka jana, Serikali kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na  Mazingira, January Makamba alipiga marufuku moja kwa moja, utengenezaji, usambazaji, uingizaji na matumizi ya mifuko ya plastiki nchini kuanzia mwaka huu. Makamba alisema mifuko ya plastiki imekuwa na changamoto kubwa ya mazingira kwa kuwa sehemu kubwa ya mifuko hiyo hutolewa bure na kusambaa ambapo husababisha  mafuriko na athari nyingine kubwa za kimazingira. Anasema ofisi yake inakamilisha majadiliano ndani ya serikali na baadae kuwahusisha wadau kuhusu dhamira ya kupiga marufuku moja kwa moja matumizi ya mifuko ya plastiki nchini. Anasema serikali itatoa muda kwa waliojiajiri na kuajiriwa kwenye biashara ya mifuko ya plastiki kujiandaa kuacha shughuli hizo na itawezesha mazingira ya utengenezaji na upatikanaji wa vifungashio mbadala.  “Tumetuma wataalamu wa serikali katika nchi zilizofanikiwa kwenye jambo hili ili kujifunza namna bora ya kulitekeleza jambo hili,” anasema Makamba. Nchi ya Rwanda na  Zanzibar zimefanikiwa katika upigaji marufuku wa mifuko ya rambo baada ya kuonekana ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira na mafuriko kutokana na mifuko hiyo kuziba katika mitaro. Licha ya serikali kupiga marufuku matumizi ya mifuko plastiki, vyombo vya plastiki aina ya sahani, bakuli, vikombe vimeendelea kutumika huku viwanda vikizidi kuvizalisha kwa wingi hivyo kufanya afya ya mwanadamu kuwa hatarini kukumbwa na magonjwa ya saratani. Walter Miya ni Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya Marafiki wa Watoto wenye Saratani Tanzania, anasema plastiki imetengenezwa kwa kemikali zaidi ya 200 ambazo  zinaweza kusababisha aina 100 za saratani. Anasema toka matumizi ya plastiki yazidi kuongezeka nchini, ugonjwa wa saratani nao umeongezeka  hasa kwa upande wa akina mama  ambapo ugonjwa huu huharibu ukuaji wa mfumo wa uzazi hususani kwa watoto ambao bado hawajazaliwa, mabadiliko ya kijenetiki, matatizo ya kushindwa kuona, uyeyushaji wa chakula tumboni kuwa wa tabu au kutokamilika na ini kushindwa kufanyakazi vizuri. Anasema kutokana na utafiti mdogo walioufanya inaonesha kuwa asilimia 60 ya saratani zimesababishwa na matumizi ya vifaa vya plastiki. “Watu wengi wanatumia vifaa vya plastiki bila kujua madhara yake, ukienda majumbani utakuta wanawake wengi wanachemsha maji na kuyahifadhi katika ndoo za plastiki yakiwa bado ya moto. “Baada ya muda ukija kuchunguza ile ndoo utakuta ina mabaka mabaka maana yake imeshatoa kemikali nyingi na athari hutoiona kwa muda huu, mpaka ifike miaka 10 au 15 na ndio maana huwezi kugundua saratani yako imesababishwa na nini,” anasema Miya. Anasema pia kuna kinamama ambao hutumia mifuko ya rambo kufunikia wali wakati wa kupika ili uweze kuiva haraka bila kujua kuwa mifuko  hiyo ina athari kubwa kutokana na kemikali zilizopo kuingia katika chakula hicho. Miya anasema jamii inapaswa kupunguza matumizi ya plastiki au kutumia zilizo na viwango ambavyo hazitoleta madhara na kwa upande wa wachemshao maji wanapaswa kusubiri hadi yapoe ndipo wamimine katika ndoo. “Licha ya jitihada zinazoendelea kufanywa na watu mbalimbali, bado jamii haina uelewa kuhusiana na vifaa hivyo vya plastiki. “Hivi karibuni kuna taarifa ilisambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa watu wasitumie vikombe vya plastiki, sahani, bakuli na hata mifuko ya rambo katika matumizi ya vyakula, lakini ukipita mitaani utakuta bado wanaendelea navyo,” anasema Miya. Anasema kuna vitu vingi ukiviangalia unaweza ukaogopa ila huwezi kuvikimbia ni kuangalia ni namna gani tunaweza kuvipunguza ili athari ya saratani isizidi kuongezeka. “Binafsi natembea na kontena langu la aina ya glass ili kuweza kuhifadhia chakula pindi ninapoenda kununua , nimeamua kutembea nalo kutokana na mama lishe wengi kutumia vyombo vya plastiki katika kuwekea chakula,” anasema.  “Kutokana na kukithiri kwa matumizi ya  plastiki wakati serikali ilipiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki, tunahitaji sera na sheria dhidi ya matumizi ya vifaa hivi. “Inatakiwa iwepo sera ya kutoruhusu kusafirisha maji bila kuwa na vifaa vinavyodhibiti joto kama wafanyavyo wanaposafirisha maziwa,” anasema Miya. Anashauri iwepo sheria ya kuwadhibiti wauzaji wa  maji juani kuanzia asubuhi hadi jioni kutokana na kupata kemikali nyingi inayotoka kwenye chupa za plastiki kwa sababu ya kuwapo juani kwa muda mrefu. 
0
MATUMIZI yasiyo sahihi ya mihuri ya wenyeviti wa vijiji na mitaa yameendelea kuwaumiza wananchi kutokana na kutozwa fedha pale wanapohitaji huduma hiyo kwenye ofi si hizo.Hali ni mbaya zaidi kwa wananchi wenye hali duni za maisha ambao baadhi wameshindwa kupata huduma za mihuri kwenye barua au fomu za maombi na kuuza mali za familia kugharamia. Wakazi wa Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya waliohudhuria Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Maadili kwa Watumishi wa Umma kata ya Kyimo wamedai hayo wilayani hapa karibuni.Maonesho hayo yaliandaliwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Diwani wa Viti maalumu kata ya Kyimo, Emmy Masseta alisema bado wananchi wengi vijijini hawatendewi haki na wenyeviti wa vijiji wanaowataka walipie huduma ya kugongewa mihuri na kuhoji msimamo wa serikali katika jambo hilo ni upi.Mkazi wa Kijiji na Kata ya Kyimo, Marley Mwabulambo alisema mwenyekiti wa kijiji chao amekuwa akiwatoza Sh 3,000 na zaidi akigonga mhuri kulingana na kipato cha mtu. “Kuna haja ya kuwatazama kwa jicho la tatu wenyeviti wetu kwani wapo baadhi hata wanaposhughulikia suala la mauziano ya ardhi, asilimia 10 ya fedha inayotakiwa kupelekwa kwenye halmashauri ya kijiji haionekani na pia waliohusika kulipa asilimia hiyo hawapewi stakabadhi.Kwanza mwananchi kutozwa huduma ya muhuri ni sheria?” Alihoji Mwabulambo. Akijibu hoja hizo, Mkuu wa Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Paul Kanon alisema msimamo wa serikali ni mihuri yote kuwa chini ya watendaji wa mitaa, vijiji na kata na si wenyeviti wa vitongoji akisisitiza kuwa huduma ya kugongewa mihuri inapaswa kuwa bure si malipo.Aliwataka wananchi kutambua ofisi za mitaa na vijiji zinaendeshwa kwa kasma ya serikali na si fedha zitokanazo na kuchangishwa, hivyo huduma zinapaswa kutolewa bure huko.“Serikali ilitangaza mihuri iwe chini ya maofisa watendaji na si wenyeviti. Mwenyekiti wa mtaa au kijiji na Ofisa Mtendaji wakitoza fedha za muhuri ni ukiukaji maadili ya utumishi wa umma hivyo msilipe pesa kupewa huduma,” alisisitiza Kanon.Akitoa mada ya Maadili ya Utumishi wa Umma kwenye maadhimisho, Ofisa Maadili Ofisi ya Sekretarieti ya maadili ya utumishi wa umma Kanda, Gideon Mwafili aliwataka wananchi kutofumbia macho maovu yanayofanywa na viongozi wao.Alisema maeneo ya vijijini kwenye mizizi ya serikali kuna malalamiko ya uwajibikaji wa watumishi wa umma na viongozi, jambo ambalo likipuuzwa lina mchango mkubwa kuporomoka maadili ya viongozi na watumishi wa serikali ngazi za juu.Akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Chalya Julius kwenye maadhimisho hayo, Ofisa Tawala wilayani hapa, Amimu Mwandelile aliwataka wananchi wanapowataja viongozi wasio na maadili wawe na uzalendo na kutaka wanaoifuata wapewe haki stahiki na kuwaongezea moyo wa kujituma kazini.
3
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga siku mbili mfululizo kusikiliza kesi ya uchochezi inayowakabili vigogo tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ikiwemo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe.Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko jana walifika mahakamani hapo wakitokea uraiani baada ya kukaa gerezani kwa miezi minne. Kesi hiyo ambayo imepangwa kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, amepanga kusikiliza shauri hilo kwa siku mbili mfululizo.Wakili wa Serikali, Wankyo Simon alidai kuwa kesi hiyo ililetwa mahakamani hapo jana kwa ajili ya kutajwa. Hakimu Simba aliieleza mahakama kuwa, amepewa maelekezo jana asubuhi kuwa shauri hilo limepangwa mbele yake kwa kuwa Hakimu aliyekuwa akisikiliza awali amebadilishiwa kituo cha kazi.Kesi hiyo awali likuwa ikisikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Wilbald Mashauri ambaye sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu. Hakimu alieleza kuwa kesi hiyo itaendelea pale ilipoishia na aliutaka upande wa mashitaka kuwasomea upya washitakiwa mashitaka yanayowakabili ambayo waliyakana.Baada ya kusomewa mashitaka hayo, Wakili Simon aliiomba mahakama irejee uwamuzi wa mahakama kuu kwamba shauri hilo lisikilizwe haraka iwezekanavyo. Wankyo alimuomba na hakimu apange tarehe ya kuanza kusikiliza kesi hiyo ili walete mashahidi. Wakili wa utetezi, Profesa Abdalah Safari aliiomba mahakama ipange tarehe za usikilizwaji kulingana na kalenda yao kwa kuwa wana kesi zingine katika mahakama kuu na wameshalipwa. Hata hivyo, Hakimu Simba alikataa ombi hilo kwa kuwa kesi hiyo inawakili wengine wa utetezi hivyo wanaweza kumwakilishwa.“Hatuwezi kupanga tarehe kulingana na kalenda zenu nyie mawakili, kama wewe hautakuwepo mawakili wenzio watakuwakilisha, sheria inaelekeza kesi zisikilizwe mapema ili ziishe,” alieleza Hakimu Simba. Baada ya maelezo hayo, Hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 28 na 29 mwaka huu kwa ajili ya kusikiliza mashahidi wa upande wa mashitaka.Mbali ya Mbowe washitakiwa wengine ni Katibu Mkuu Chadema Taifa, Dk Vincent Mashinji, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Chadema Taifa, Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Katibu Mkuu Taifa, Vicent Mashinji, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, John Heche na Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya.Washitakiwa wanakabiliwa na mashitaka 13 likiwemo la kula njama, ambapo wote wanadaiwa kuwa, February 1 na 16, 2018, Dar es Salaam walikula njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali na kukiuka tamko kutawanyika.Wanadaiwa Februari 16, mwaka jana katika viwanja vya Buibui na Mwananyamala Kinondoni wakiwa walikusanyika na azma ya pamoja, waliitekeleza kwa kufanya mkusanyiko usio halali na kusababisha watu waogope kuwa watakwenda kupelekea uvunjïfu wa aman Pia wanadaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana katika barabara ya Kawawa Kinondoni Mkwajuni washitakiwa hao wakiwa na wenzao 12 ambao hawapo mahakamani walikiuka tamko la kuwataka kutawanyika la Afisa wa polisi SSP, Gerald Ngiichi kwa kugoma kutawanyika na kupelekea uvunjifu wa amani.Inadaiwa kugoma huko kulipelekea hofu na hatimaye kusababisha kifo cha Akwilina Akwilin na majeruhi kwa askari wawili ambao ni H.7856 PC Fikiri na E.6976 CPL Rahim Msangi. Katika mashitaka mengine ya uchochezi wa uasi linamkabili Mbowe, anadaiwa Februari 16, mwaka jana katika maeneo Dar es Salaam, alitoa matamshi ya kupandikiza chuki na dharau kwa upande wa raia wa Tanzania dhidi ya mamlaka halali. Bulaya anadaiwa Februari 16, 2018 katika viwanja vya Buibui wilayani Kinondoni, Dar es Salaam alïtenda kosa la kukaidi amri halaĺi ya tamko la Jeshi la Polisi.
3
Na BEATRICE KAIZA HAITHAMKIM ni msanii wa kike anayepanda kwa kasi kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, jina lake kamili ni  Haitham Ghazal ambaye yuko chini ya lebo ya MJ Records, Mrembo huyo ngoma yake ya kwanza inaitwa ‘Fulani’ aliyomshirikisha rapa mkongwe wa Bongo fleva, Mwana FA ambaye inafanya vema ndani na nje ya nchini. Na sasa anakuja na kazi yake mpya aliyomshirikisha mrembo wa duania Wema Sepetu na kummwagia sifa  lukuki  kuhusu mrembo kufanya  kazi yao mpya ambayo Wema Sepetu ameimba. ‘’Wema Sepetu ni msanii tena anakipaji cha kuimba kama mimi kusema ukweli tumefanya kazi zuri na itakuwa tishio kwa wasanii wa kike ambao wametutangulia kwenye gemu,’’ alisema  Haithamkim. Ngoma hiyo itwayo ‘PlayBoy’ ambayo ipo jikoni, mwanadada Haitham amesema kuwa tangu aingie kwenye tasnia hii ya muziki hajawai kuona wimbo ambao unampa furaha kila kukicha. ‘’Naomba mashabiki zangu wakae mkao wa kula kwani PlayBoy ni wimbo ambao mwaka 2017 ni lazima upate tuzo, sio kama najisifia hapana ni kutokana na maandalizi ya wimbo huo,’’. Akizungumza na Swaggaz, mkali huyo anasema kuwa kitu cha kumshukuru Mungu ni lebo yake na prodyuza wake kwa kazi mzuri kwa kumtengenezea wimbo ambao utakuwa ni tishio ya wasanii wa hapa nyumbani. ‘’Daxo Chali ni kiongozi wangu ambaye ananetengenezea ngoma zangu pia kitu cha kujivunia ni kuwa msanii wa kike ninaefanya vema kutokana na MJ Records kunipika vema na kunipa mafunzo ya kutosha katika tasnia hii ya muziki. Asante uongozi wangu kwa kuniweka katika uangalizi mzuri zaidi ili niweze kufanya kazi nzuri na kutimiza malengo yangu ya kuwa msanii bora ndani na nje ya nchi. SWAGGAZ: Kwa nini umshirikishe Wema Sepetu na siyo mtu mwingine? HAITHAMKIM: Kwanza kabisa, aina ya Bongo Fleva ninayoimba mimi ni mpya, unaitwa Tropical House. Baada ya mimi kumaliza kuingiza vocal kwenye ngoma hiyo, kulingana na aina ya wimbo wenyewe, menejimenti yangu ilipendekeza Wema Sepetu akae kwenye ngoma hiyo ndipo itanoga zaidi. SWAGGAZ: Wema Sepetu anakipaji cha kuimba kweli? HAITHAMKIM: Nasema hivi kipaji chake  mtakijua kwenye prayBoy siwezi kusema mengi na mashabiki wangu watajionea wenyewe. SWAGGAZ: Siku ambayo umeambiwa kuwa unakwenda kufanya kazi na Wema Sepetu ulijisikia je? HAITHAMKIM: Siku ambayo niliambiwa kuwa ninafanya wimbo wangu mpya na Wema Sepetu sikutegemea kuwa atafanya vizuri kama alivofanya, kusema kukweli ni wimbo mzuri zaidi ya nyimbo zote kwani Wema anafanya poa na mimi mwenyewe nimefanya poa zaidi. SWAGGAZ: Nini kinafanya kichupa cha PrayBoy kisitoke wakati kipo tayari? HAITHAMKIM: Kichupa kipo tayari, kwa hiyo kinachosubiliwa ni siku ifike, maandalizi yamesha fanyika na video tunatarajia kuiachia mwanzoni kwa mwaka 2017,lakini mitandaoni hasa YouTube itaanza kuonekana hivi karibuni.   SWAGGAZ: Sawa ni changamoto gani  ambazo unakutana nazo mara kwa mara katika tasnia hii? HAITHAMKIM: Changamoto ambayo hadi sasa inanisumbua kichwa ni wakati mwingine ninapokuwa ninasukuma kazi zangu kwenye media kuna baadhi ya watangazaji na Madj ni wasumbufu,  kwani wananitaka kimapenzi pia kwa sababu ninajielewa na ninajua nini nafanya ninaweza kupapana nao na hazinikatishi tamaa. SWAGGAZ: Kuna tetesi zinasema kuwa unamahusiano ya kimapenzi na Mirror msanii wa Bongo Fleva ambaye ni zao la Endless Fame inayomilikiwa na Wema Sepetu na h ii ndio imekufanya hadi ukaweza kumpata Wema Sepetu na kuweza kufanya nae kazi? HAITHAMKIM: Sio kweli mimi na Mirror ni marafiki tu na hatuna uhusiano zaidi ya urafiki na kuhusu Wema ni menejimenti yangu ndio ilimtafuta Wema na sio mimi. SWAGGAZ: Asante sana Haithamkim kwa ushirikiano wako. HAITHAMKIM: Asante polisi wa Swaggaz, nakutakia siku njema na kazi njema. Asante uongozi wangu kwa kuniweka katika uangalizi mzuri zaidi ili niweze kufanya kazi nzuri na kutimiza malengo yangu ya kuwa msanii bora ndani na nje ya nchi.
1
KUELEKEA siku ya ukimwi duniani, msanii maarufu wa muziki wa kufoka foka nchini Karama Masoud ‘Kalapina’ amesema anashangaa wasanii ambao wanadai hawatumii dawa za kulevya lakini wanasuasua kutumia mipira ya kiume ikiwa ni kujilinda na maradhi ikiwemo mambukizi ya Ukimwi.Kalapina alisema hayo katika semina ya wasanii iliyoandaliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamini Mkapa Foundation iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ambapo alisema ikiwa kuna msanii hatumii kinga kujilinda hana tofuati na anayetumia dawa za kulevya.“Kwenye tasnia ya sanaa ni rahisi kupata mambukizi ya HIV kwa kuwa wasanii wanazungukana humu humu, mdada bongo movie anatembea na msanii wa bongo fleva, mbaya zaidi wanaunganisha mkanda yaani anatoka kwa huyu anaenda kwa yule,” amesema.Amesema vita ya mapambano ya ukimwi kwa wasanii itafanikiwa iwapo tu wataacha kunyanyapaa wenzao wanaotumia madawa ya kulevya na kuwasaidia kutoka kwenye uraibu huo.“Hatuwezi kupambana na ukimwi bila kuwapambania wenzetu walioathirika na dawa za kulevya ili watoke huko, matibabu yapo tuwasaidie, tusiwanyanyapae,” alisisitiza Kalapina.Wakati Kalapina akisema hayo, gwiji wa mipasho katika muziki taarabu Khadija Kopa amesema elimu zaidi kwa wasanii chipukizi hususani wa kike inahitaji kutolewa, kwani wengi wanaoingia kwenye tasnia hiyo wanajikuta wanaingia kwenye makundi yasiyofaa.“Kuna msemo kwa wasanii wanaita kuunganisha mkanda, wengi wanaunganisha mkanda anatoka kwa huyu anaenda kwa yule tukianza kupukutika tutaisha kweli, hasa vijana wakishapiga alkasusu wanataka kukomoa, hawandaani, mtakwisha nawambia,” amesema Kopa.Naye msanii Hamis Mwinjuma ‘Mwana Fa’ alisema ni muhimu kwa wasanii kupima na kujua afya zao na kujilinda na kuwa makini katika mwenendo wa maisha na kuishi kwa utaratibu.Kwa mujibu wa takwimu za serikali zilizotolewa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu hivi karibu amesema vijana ndio kundi kubwa linaloongoza kwa mambukizi mapya, ambapo vijana 65,000 uambukizwa kila mwaka nchini.Ummy alisema kuwa vijana wenye umri wa miaka 10 mpaka 19 na wale wa miaka 15 mpaka 24 ambapo asilimia 84 ni wasichana na asilimia 20 ni wavulana ndio wathirika wakubwa. Alisema pia changamoto kubwa iliyopo kwa sasa ni wavulana asilimia 90 hawapimi VVU.Hata hivyo, Ummy alisema serikali imeweka mkakati wa kupambana na ugonjwa huo kwa kuingiza dawa za kisasa za kufubaza vijidudu vya ukimwi, na kuongeza vituo vya afya ya mama na mtoto kutoka 3,500 vilivyokuwepo hadi vituo 4,000 kwa sasa.Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2016 na 2017 zinaonyesha Tanzania mambukizi ya virusi vya ukimwi bado upo kwa kiwango cha juu.Takwimu hizo zinaonesha watu takribani milioni 1.4 wanakadiriwa kuishi na irusi vya ukimwi nchini na wengine 81,00 hupata maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi kila mwaka sawa na watu 222,000 kila siku na waathirika wakubwa wa janga hilo wakiwa ni wasichana.Mkurugenzi wa Taasisi ya Benjamini Mkapa, Ellen Senkoro alisema kundi la vijana ndio linalokabiliana na vishawishi hatarishi hususani katika maambukizi ya Ukimwi na huduma nyingine za ugonjwa huo.Alisema taasisi yake kwa kushirikiana na wizara wamekua wakibuni mbinu mbalimbali ili kuwafikia vijana katika kuchochea mabadiliko chanya ya tabia kwa ujumla kwa vijana kwa kukabili nyanja zote za maisha zinazomzunguka kijana.
3
NA MWANDISHI WETU-MACHAKOS TIMU ya soka ya Tanzania Bara  ‘Kilimanjaro Stars’ imeondolewa kwa aibu katika michuano inayosimamiwa na Baraza la Vyama vya Soka Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ‘CECAFA’ baada ya kukubali kichapo kingine cha bao 1-0 kutoka kwa timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’. Kilimanjaro Stars imeondolewa katika michuano hiyo ikiwa iinashika mkia katika kundi lake A  baada ya kujikusanyika pointi moja,kupitia michezo minne, ikitoka sare mchezo mmoja na kuruhusu kufungwa michezo mitatu. Katika mchezo wa jana dhidi ya Kenya, Kiliman jaro  Stars ilicheza soka lisilokuwa na ladha na kuiruhusu bao  dakika ya 19 kupitia kwa Vincent Ouma Oburu, baada ya beki wa Kilimanjaro Stars,Kenedy Wilson kuchelewa kupokea mpira wa pasi na matokeo yake kuwahiwa na mfungaji. Bao hilo lilidumu hadi dakika 45 za kwanza zilipomalizika,kipindi cha pili mambo yalibadilika huku timu zote zikishambuliana kwa zamu. Mara kadhaa mashuti ya mshambuliaji wa Kilimanjaro Ibrahim Ajib, yaliokolewa na  kipa wa Kenya, Patrick Matasi. Kadri muda ulivyosonga Kenya walizidisha mashambulizi langoni mwa Kilimanjaro Stars yaliyowaongezea  presha vijana wa kocha, Ammy Ninje ambao walionekana kupokonywa mipira kirahisi na wapinzani wao hao. Katika mchezo huo,Ninje alifanya mabadiliko kadhaa kwa kuwaingiza chipukizi, Yahaya Zayd na Aman Kyata, lakini hawakuweza kutengeneza nafasi yoyote ya kuweza kupata bao la kusawazisha. Kwa matokeo hayo sasa Kenya anaungana na Zanzibar kutinga hatua ya nusu fainali, licha ya Zanzibar kupoteza mchezo wake dhidi ya Libya kwa bao 1-0.   Ushindi huo uliifanya Libya kufikisha pointi sita,lakini haukuisaidia isiondolewe katika michuano hiyo baada ya kuzidiwa pointi moja na Kenya ambayo ilifikisha pointi saba kutokana na ushindi wake dhidi ya Kilimanjaro Stars.  Kutoka kundi B, Uganda na Burundi zimefuzu nusu fainali ya michuano hiyo,hivyo kuungana na Zanzibar Heroes na wenyeji Kenya. Ratiba ya fainali inaonyesha kuwa nusu fainali ya kwanza itachezwa Desemba  14, ambapo Kenya watacheza na Burundi, wakati nusu fainali ya pili itafanyika desemba 15, ambapo Uganda watacheza na Zanzibar.
4
HOSPITALI ya Rufaa ya taifa ya Mirembe haikujengwa mkoani Dodoma kutokana na mkoa huo kuwa na wagonjwa wengi wa akili (vichaa) bali kuwepo kwa gereza la Isanga ambalo wanafungwa wahalifu wakubwa na wauaji wanaotakiwa kupimwa akili zao.Naibu Waziri wa Afya, Maendelelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile alitoa kauli hiyo baada ya Spika Job Ndugai kutaka kujua kama hospitali hiyo ya kutibu wagonjwa wa akili ilijengwa hapo kufuatia Dodoma kuwa na wagonjwa wengi wa akili.Dk Ndugulile alisema hospitali hiyo ilijengwa hapo kutokana na Dodoma kuwa na gereza la Isanga lenye wafungwa wa mauaji na wahalifu wakubwa ambao hutakiwa kupimwa akili zao.Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM) aliyetaka kujua kwa nini dawa za kifafa na ugonjwa wa akili wilayani Ulanga mgao wake ni kidogo wakati wilaya hiyo inaongoza nchini kwa kuwa na wagonjwa wengi wa maradhi hayo. Dk Ndugulile alisema ni kweli Morogoro hasa wilaya ya Ulanga kuna wagonjwa wengi wa kifafa na akili, lakini atafuatilia kujua kwa nini dawa hizo hazifiki huko wakati zipo za kutosha.Akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Njombe Mjini, Edward Mwalongo (CCM) aliyetaka kujua serikali inajipangaje kuwatibu, kuwapa mavazi na makazi wagonjwa wa akili mitaani. Dk Ndugulile alisema wizara inaendelea kuimarisha huduma za afya nchini ikiwemo huduma ya afya ya akili. Uimarishaji huo wa huduma ya afya ya akili unakwenda hadi ngazi ya afya ya msingi ambako ndiko jamii ilipo.“Pamoja na kuongezeka kwa wagonjwa wa akili wanaorandaranda barabarani, sheria ya afya ya akili ya mwaka 2008 inawataka ndugu na jamii kuibua wagonjwa wa akili na kuwapeleka vituo vya kutolea huduma wapewe tiba,” alisema. Alisema wagonjwa wakipata nafuu, huruhiswa kukaa na familia zao na jamaa zao. Jukumu la kwanza la kulinda afya ya jamii huanzia ngazi ya familia, lakini jamii zinawanyanyapaa, kuwabagua, kuwatenga hivyo kuranda mitaani.
3
Meneja Mkuu wa Shirika hilo, Florens Seiya alisema hayo jana wakati akizungumza na HabariLeo na kuongeza kuwa soko litakalofanyiwa marekebisho ni soko dogo huku lile la shimoni likibakia kama lilivyo likiwa kama ni ukumbusho.Alisema soko hilo litafanyiwa maboresho kulingana na mahitaji ya sasa kwani limekuwepo kwa muda mrefu tangu mwaka 1974 likiwa na wafanyabiashara 800,000 na kwa sasa lina wafanyabiashara wanaofikia milioni tano.“Wengi sana wanategemea hili soko kwa bidhaa mbalimbali, huduma zimepanuka kukiwa na vyakula mbalimbali na aina nyingi za pembejeo,” alisema Seiya na kuongeza kuwa lengo la maboresho ni kujenga soko kubwa litakalokidhi matakwa.Alisema pindi ujenzi ukianza, Shirika hilo litatoa mkataba wa makubaliano kwa wafanyabiashara waliomo katika soko hilo ili kupisha ujenzi na pindi ukikamilika wao ndio watakaopewa kipaumbele cha kurejea.Alisema hadi kufikia Machi mwaka huu Shirika hilo litaeleza kuhusu picha halisi ya ujenzi huo kwa maana unaanza lini huku wakiwa wanatoa taarifa kwa watu wao wanaohusika kwani hawawezi kufanya lolote bila kuwajulisha.
5
Leo Baraza la Sanaa nchini (BASATA) limemfutia usajili Msanii wa Bongofleva nchini Tanzania, Dudubaya, mwenyewe amelishukuru na kusema anasubiri kupata barua ili asonge mbele kisheria. Dudubaya amefungiwa kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni kauli zisizo na staha katika vipande vyake video vya video vinavyosambaa mtandaoni, hata hivyo katika vipande hivyo kuna wakati alikuwa akiikosoa Basata. Basata ilipomtaka kuripoti leo saa 4:00 asubuhi ya leo Januari 7, 2020 kwa ajili ya kwenda kuhojiwa zaidi lakini alikaidi amri hiyo na kujibu haendi kwakuwa haoni kosa alilolitenda. Kitendo hicho kilichowafanya Basata kupitia tamko lililosainiwa na Katibu Mtendaji wake,Godfrey Mngereza kutangaza kumchukulia hatua ya kufuta usajili wake kwa kile walichoeleza ameidharau taasisi hiyo yenye dhamana la kuwasimamia wasanii ikiwemo suala zima la maadili yao. Hata hivyo Dudubaya amesema tangazo hilo na yeye kaliona mtandaoni lakini hajapewa barua rasmi “Kama ni shoo nitapiga kama kawaida hata leo nikipata mpaka pale watakaponipa barua ili niwasiliane na mwanasheria wangu tuone nini la kufanya kwani kama ni kulipa kodi nalipa na hata mfanyakazi hafukuzwi bila kupewa barua,acha tuonyeshane tukutane mahakamani, tumechoka sanaa hii kuchezewa,”amesema. Hata hivyo kupitia ukurasa wa Instagramu Basata walipost tangazo la kumfutia usajili Dudubaya naye alicomment kwa kuandika kuwa anawashukuru kwa kushiriki.
1
MKOA wa Dodoma unaweka mkakati wa kuvutia watalii kutembelea mbuga ya Ruaha kupitia njia ya mkato ya kuingia kwa kupandisha hadhi barabara ya Mpunguzi hadi Ilangali kilometa 95, badala ya kuzunguka njia ndefu ya Mtera, Iringa hadi Ruaha.Akizungumza katika mikutano miwili ya hadhara miwili katika kijiji cha Ilangali na Manda vilivyopo katika kata ya Manda wilayani Chamwino, Mkuu wa Mkoa, Dk Binilith Mahenge alimtaka Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) wilayani Chamwino, Makandi Mange kuipa kipaumbele barabara hiyo wakati akitenga fedha za kuboresha barabara.Dk Mahenge alimuagiza Mange kupanga bajeti ya kutengeneza barabara kwa kiwango cha changarawe kwa lengo la kuwapa unafuu watalii kutoka Dodoma kutembelea hifadhi hiyo lakini pia kupata mapato ya halmashauri hiyo.Alitoa maelekezo hayo na kumtaka Mange kuleta mapendekezo yake katika kikao cha bodi ya barabara kinachofanyika mwisho wa mwaka kikiwa na mpango wa namna ya kuboresha barabara hiyo.Maagizo hayo yalitolewa baada ya wananchi wa vijiji viwili kumlalamikia mkuu huyo wa mkioa kwamba barabara hiyo ni mbaya, lakini mkoa ungeweza kuiboresha na kutumiwa na watalii kwa ajili ya kufika kwenye hifadhi na kuiongezea halmashauri mapato.Mkazi wa Kijiji cha Manda, Michael Semamba aliuliza serikali ina mkakati gani kutengeneza barabara hiyo hadi katika lango la mbuga ya Ruaha ili kupata mapato kutokana na watalii kutembelea hifadhi hiyo.Cosmas Ulaya wa kijiji cha Manda, alihoji kwamba serikali inaonaje kutengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe ili kupitika wakati wote kutokana na hali yake mbaya kwa sasa.Mwananchi Kaneni Mgimwa aliomba kutengeneza barabara hiyo umbali wa kilometa 95 kutoka Mpunguzi hadi Itengule ili kuongezeka magari ya abiria badala ya sasa ambapo ni gari la kampuni moja ndilo linapita huko na kujaza watu kupita kiasi.Alisema kutokana na ubaya wa barabara hiyo, kumechangia kuwa na basi moja ambalo linajaza abiria kupita kiwango na hivyo kusababisha kufika mjini wakiwa wamechafuka kutokana na kuminyana ndani ya gari.John Petro alimuomba mkuu wa mkoa kuiboresha barabara hiyo na kuipandisha hadhi ili kutumiwa na watalii kutoka Dodoma kwenda Ruaha badala ya kutumia njia ndefu ya kuzunguka Mtera, Iringa hadi kwenye hifadhi hiyo.Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa kijiji cha Ilangali kilichopo umbali wa kilometa 137 kutoka makao makuu ya wilaya, waliomba barabara hiyo muhimu katika usafiri ijengwe kwa kiwango cha changarawe kwa ajili ya kuwasaidia kusafiri na kusafirisha mazao yao.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chamwino, Samwel Kawea alimuomba Dk Mahenge kuwasaidia kuipandisha hadhi barabara hiyo ili itengenezwe kwa kiwango cha changarawe kutokana na umuhimu katika utalii na usafirishaji abiria na mazao.Akizungumza na Meneja wa Tarura aliahidi kwenda kuandaa bajeti kwa ajili ya barabara, lakini kipaumbele kinatakiwa kuwa barabara hiyo ambayo ina umbali wa kilometa 95 kutoka Mpunguzi hadi Mlangali.Mkuu wa mkoa aliwataka watendaji wa halmashauri, akiwemo mbunge na viongozi wote kupigania kutengenezwa kwa barabara hiyo na katika mkutano wa bodi ya barabara utakaofanyika mwezi Desemba wanatakiwa kuwa na ajenda hiyo.
5
WANANCHI 875 wamepatiwa huduma ya macho bure baada ya kubainika idadi kubwa ya watoto wenye umri wa kuanzia miaka mitatu hadi minane na kuanzia miaka 45 na kuendelea Babati mkoani Manyara ndio wanasumbuliwa na magonjwa ya macho kwa kiasi kikubwa.Hayo yalibainika jana wilayani Babati baada ya watoto na wazee wengi kujitokeza kupata matibabu ya macho bure na Lion’s Club ya Arusha katika kituo cha afya cha Magugu.Huduma hizo zilikuwa zikitolewa kwa siku mbili kwa ufadhili wa msikiti wa dhehebu la Kalasinga katika sherehe za maadhimisho ya miaka 550 tangu kuanzishwa na Guru Nanak.Akizungumza wakati wa majumuisho, Katibu wa klabu hiyo, Chief Maswanya alisema wametoa huduma za matibabu ya macho kwa wananchi Babati na kuwapa dawa, miwani na kuwafanyia upasuaji waliokutwa na matatizo.“Idadi kubwa ya watu wamejitokeza kupata huduma hii ya macho, wengi wao waliokutwa na matatizo ya macho ni watoto wa miaka miaka mitatu hadi minane na wazee miaka 45. Kupitia takwimu za waliohudhuria tumeona kuna watu wengi wenye matatizo ya macho na hawana elimu kujikinga na ugonjwa,” alisema.Alieleza watu waliofanyiwa vipimo kwa siku mbili ni 875, kati ya hao 714 walipatiwa dawa, 632 miwani na 102 walikutwa na mtoto wa jicho na kufanyiwa upasuaji, huku wanne wakipewa rufaa hospitali ya rufaa ya KCMC.Alisema, watu wengine sita waliandikiwa barua kwenda kufanyiwa uchunguzi katika hospitali ya Mtakatifu Elizabeth iliyopo jijini Arusha.
3
Akizungumza na gazeti hili mratibu wa bonanza hilo, Deo Lucas, alisema bonanza hilo litajumuisha vyuo vya elimu ya juu vilivyopo katika mkoa wa Dar es Salaam.“Tutafanya bonanza ambalo litashirikisha vyuo vyote vya elimu ya juu tukiwa na lengo la kujiandaa na ligi ya vyuo ambayo tutatangaza baadae yataanza lini,” alisema Lucas.Pia alisema baadhi ya vyuo ambavyo vitashiriki ni CBE, DIT, Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Chuo Kikuu cha Ardhi (AU), Chuo Kikuu cha St. Joseph Tanzania (SJUIT), Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO), Taasisi ya Ustawi wa Jamii (ISW) na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.Vingine ni Chuo cha Utumishi wa Umma Magogoni, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Utawala wa Kodi (ITA), Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) na Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ).Tanzania ilipata timu ya taifa ambayo ilishiriki katika michuano ya Afrika ya mpira wa miguu wa ufukweni iliyofanyika Shelisheli mwaka jana, lakini ilitolewa katika hatua ya pili na Misri.
4
['Manchester United inajiandaa kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, kwa Real Madrid au Juventus mwezi huu, lakini wanataka £150m. (Express)', 'Manchester United inapania kuwanunua viungo wa kati wa Aston Villa Jack Grealish, 24, na James Maddison, 23, kutoka Leicester. (Independent)', 'Wachezaji wengine wanolengwa na United ni kiungo wa kati wa Juventus na Ujerumani Emre Can, 25, na Sean Longstaff, 22, wa Newcastle. (ESPN)', 'Aston Villa ina mpango wa kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Michy Batshuayi, 26, kwa lengo la kumpatia mkataba wa kudmu. (Footmercato - in French)', 'Villa pia wanamtaka mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Olivier Giroud, 33. (Sun)', 'Mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 30, ameelezea kujitolea kwake kwa Arsenal na kutuliza tetesi za kuondoka kwake mwezi Januari. (Evening Standard)', "Arsenal imeingia katika kinyang'anyiro cha kumsaka beki wa Bournemouth na Uholanzi Nathan Ake, 24. (Telegraph)", 'Inter Milan ni moja ya klabu zilizowasiliana na wawakilishi wa kiungo wa kati wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen. Kandarasi ya kiungo huyo wa miaka 27 inakamilika msimu huu wa joto. (Sky Sports)', 'Manchester City inatarajiwa kurefusha kwa mwaka mmoja mkataba wa kiungo wa kati wa Brazil Fernandinho, 34. (Sun)', 'Dau la Chelsea la yuro milioni 40 la kumnunua mshambuliaji wa Ufaransa Moussa Dembele ,23, limekataliwa na Lyon. (Footmercato - Kwa Kifaransa)', 'Aston Villa inatafakari uwezekano wa kuweka dau la kumnunua kipa wa Stoke City Muingereza, Jack Butland, 26. (Mail)', 'Ajax imesitisha mpango wa kumnunua beki ya Tottenham na Ubelgiji Jan Vertonghen kwa sababu bei ya mchezaji huyo wa miaka 32 ni ghali sana . (De Telegraaf - Ujerumani)', 'Southampton wanataka kumsaini beki wa Valladolid raia wa Ghana Mohammed Salisu, 20. (Sky Sports)', "Leicester imeipiku Arsenal katika kinyang'anyiro cha usajili wa beki wa Juventus na Italia, Daniele Rugani, 25. (Express)", 'Arsenal imemuulizia winga wa Atletico Madrid na Ufaransa Thomas Lemar, 24. (Marca - ya Uhispania)', 'Real Madrid imewasiliana na wawakilishi wa mshambuliaji wa Liverpool na Senegal Sadio Mane, 27. (Le10Sport)', 'Manchester United na Tottenham wanatarajiwa kukabiliwa kwa ushindani mkali wa kumnunua kiungo wa kati wa Lille Mfaransa Boubakary Soumare,20, huku ofa sita za kumnunua zikiripotiwa kupokelewa na klabu yake. (Mail)']
4
MAKALA haya yatazungumzia kidogo matatizo yanayojitokeza katika utumiaji wa lugha ya Kiswahili. Tukumbuke kuwa lugha ni chombo chetu cha mawasiliano na tunapaswa kuipiga msasa mara kwa mara kadiri inavyowezekana.Yapo makosa mengi na mengine yameshawahi kuzungumziwa lakini leo tutayataja machache hata kama tutakuwa tunarudia, kwa lengo la kuweka msisitizo tu. Katika makala haya tutazungumzia zaidi makosa ya mara kwa mara ambayo tukiyaacha yanaweza kuleta mkanganyiko kwa watumiaji wa lugha hii.Yapo maneno mengi ambayo hukosewa mara kwa mara, yapo yanayochanganywa matumizi, na yapo ambayo waandishi huyatumia bila kujua. Mfano wa makosa hayo ni yale ya kuchanganya umoja na wingi kwa baadhi ya msamiati.Makosa ya aina hii hujitokeza, kwa maneno yaliyo katika mfumo wa wingi katika uundaji wake, wengi wetu huyalazimisha yawe na mfumo wa umoja. Tuangalie maneno kama vile madhumuni, madhehebu, mafao, maadhura n.k.Umbo la maneno haya ni la wingi na hayapaswi kuingizwa katika umoja. Hivyo si sahihi kutumia neno ‘dhumuni’, ‘dhehebu’, ‘fao’, ‘adhura’ n.k. Aidha, yapo maneno yenye mfumo wa umoja ambayo baadhi yetu tunayabebesha wingi kwa lazima.Kwa mfano: neno ‘saa’ ‘dawa’, ‘shule’ ‘uamuzi’. Haya ni baadhi tu. Pia, kuna makosa mengine ya mara kwa mara ambayo baadhi ya waandishi huongeza kiambishi cha awali ‘ma’ katika maneno kuonesha msisitizo au wingi, kama vile mashirikiano, mashule, makampuni, mahusiano na kadhalika. Matumizi sahihi ya maneno haya ni ushirikiano, shule, kampuni na uhusiano.Aidha, kuna ukataji wa maneno usioleta maana iliyokusudiwa. kwa mfano, unapiga simu toka wapi badala ya unapiga simu kutoka wapi, tafsiri sisisi kutoka katika lugha nyingine kwa mfano, mwisho wa siku badala ya “hatimaye” au “mwishowe”.Kuna makosa yanayokuzwa na waandishi, haya mara nyingi huwa yanabebwa kutoka katika jamii ya wazungumzaji ambao ni wamiliki wa lugha yao, kuna maneno ambayo huwa ni simo au yaliyotoholewa bila kufuata misingi ya lugha.Makosa haya huwa yanarekebishika lakini athari zake huwa katika taarifa ambazo labda zimehifadhiwa kwa maana ya kurekodiwa au kuandikwa. Makosa hayo huonekana dhahiri wakati wa kurejea kipindi kirefu kilichopita tangu matumizi ya msamiati huo. Matumizi potofu: Kizazi cha sasa kimeibua dhana ya mfanano wa matendo, na matendo hasi zaidi, kuna upotoshaji ambao umekithiri katika jamii na kunyang’anya msamiati kwa waandishi kwa hofu kwamba akiliandika atamaanisha maana mbaya.Yaani msamiati wa kawaida umeingia shubiri, ni vigumu kwetu waandishi kutumia maneno kama kutia, kukazana, kusimika, denda, ingiza, chomeka, chomoa, jicho, ndogo, kulamba, mzigo, mate, kugonga au kugongwa. Makosa ya kiuandishi, Jamii ya wasomaji hufanya marejeo mengi kutoka katika maandiko, hivyo inapandwa mbegu ambayo hatuijui ukubwa wake na athari zake.Uundaji wa msamiati kama live, prodyuza, tyuni, nimekumisi, inaweza ikawa na nguvu badala ya mubashara, mtozi, kurahani, na nimekuhamu. Kuna maneno mengine ya Kiingereza ambayo watu wamejenga imani kwamba hayana msamiati wake katika Kiswahili, kama birthdaysiku ya kuzaliwa, surprisekushitukiza, booking- wekesho, appointment- miadi weekend-mwisho wa wiki/ juma. Tanzania ina makabila mengi sana. Inakadiriwa kuwa yapo makabila zaidi ya 120, makabila haya yana athari kubwa katika lugha ya Kiswahili.Unaweza kutambua asili ya mtu kwa lafudhi yake. Isivyo bahati ni kwamba hakuna tena kabila la Waswahili ambalo labda lingepewa jukumu la kuwa waandishi kutokana na lafudhi murua ya Kiswahili. Waandishi tumejikuta tukitumia lafudhi za makabila yetu, baadhi ya maneno ya Kiswahili yanayokinzana sana na makabila yetu.Kuna makabila hawana /r/ katika matamshi yao, unapomlazimisha kutamka neno lenye r anatamka l, wengine hawana z na badala yape hutumia s, wengine f badala ya v. Lakini pia kuna kushadidia neno kwa kuongeza ga kama kulimaga, kulaga, kusimikaga, kukimbiaga, na kadhalika. Haya ni matatizo ya lafudhi na siyo lahaja. Matatizo yaliyo katika lahaja yanatatulika kiurahisi kwa kuwa kila lahaja ina namna ya kumeza msamiati wake na hakuna makosa ya kuubadilisha msamiati tofauti na lafudhi ambayo hujenga msamiati mpya potofu unaokaribiana na msamiati sanifu.Kwa mfano: luga, singo, langi, ledio, kasa, hombi, akuna, ongera, n.k. Makosa ya kurithi, pamoja na kwamba sisi ni mahiri katika lugha ya Kiswahili na ndio maana tumepewa jukumu la kuwa waandishi, kuna makosa mengi sana ya kurithi ambayo tumeyapata na tumeyapokea, mengine kwa kulazimishwa na wanaojiita wakongwe katika tasnia na mengine yapo kwa kuwa tumeyakuta. Maneno kama vile pelekea, sintofahamu na kadhalika. Aidha, ni dhahiri kwamba upo msamiati wa kimahalia. Misamiati ya aina hii inatokana na dhana na hii inaweza kuwa inazaliwa kila siku kutokana na mazingira ya maisha tunayoishi. Hivi leo, nchi hii ina maeneo mengi sana yanayojulikana kama chekereni.Chekereni limetokana na maneno ya Kiingereza kwa maana ya check rail yaani kuwa mwangalifu/angalia reli. Mfano mwingine ni neno mlimani kwa maana ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Neno Mlimani likitamkwa peke yake kwa maana ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam halina ubishi kuwa linafahamika lakini kuna vyuo vikuu vingapi nchini ambavyo havinasibishwi na mlimani. Uundaji wa maneno kwa namna hii huwa yana historia yake na hupata mashiko makubwa katika matumizi. Ufumbuzi ni kwamba tukiwa waandishi tunapaswa kujifunza mara kwa mara, kununua machapisho, kufanya rejea, kuwasiliana na Baraza pale kunapotokea mgongano katika matumizi ya Kiswahili fasaha.
3
Huku janga la virusi vya corona likizidi kuwa tishio kote duniani, kila taifa limebuni njia mbali mbali ya kuwasadia wasiojiweza katika jamii haswa baaa ya wengi kukosa ajira. Msanii Diamond Platnamz ni kati ya wathamini waliojitokeza kuonyesha wema kwa wasiojiweza msimu huu wa Ramadhan, akiahidi kulipa kodi ya nyumba kwa familia 500. Ahadi yake hii ilimuamsha mpenziwe wa zamani  Zari aliyemshambulia kwa kuweka ahadi za uongo kwa umma. Kulingana na Zari, Diamond hawezi kujifanya kuwa ataweza kuzisaidia familia 500 katika kuzilipia kodi ya nyumba wakati ameshindwa kukidhia mahitaji ya familia yake. Ujumbe wake ukimuanika msanii huyu kuhusu jinsi alivyowatelekeza wanawe. …….na hujui wanachokula wanao, ma hata jinsi wanavyolala, ama iwapo bima ya hospitali na karo kulipwa. Hutaweza kufurahisha ulimwengu wakati wanao hawana furaha. Unaeneza uongo….,’’ Ujumbe wa Zari. Akihojiwa katika redio ya Wasafi asubuhi ya Jumatatu, Aprili, 27 kuhusu jinsi msaada wake ungefika kwa familia hizo, msanii huyu alieleza pia kuwa aliona ujumbe wa Zari mtandoni na kuchukua fursa ya kipekee kumpigia simu wakazungumza na. Alieleza kuwa anamheshimu Zari na Licha ya tofauti zao yuko tayari kuwalea wanawe. #GoodMorning • "baada ya kuona ujumbe ule wa @zarithebosslady , nilimpigia simu na kumueleza, licha ya tofauti zetu Ila bado namuheshimu Sana. Alinielewa na nadhani baada ya Corona Kuisha tutapanga namna ya kuwalea watoto wetu pamoja " – @diamondplatnumz . . Endelea kusikiliza 88.9 @wasafifm MUDA HUU mpaka saa 2:30 asubuhi na Kutazama @wasafitv, pia unaweza kufuatilia matangazo haya moja kwa moja kupitia Channel yetu ya YouTube #WasafiMedia #GoodMorning na @zembwela @rwenyagira salmadacotha @charles_william2 #HabariZaAsubuhi A post shared by Wasafi FM (@wasafifm) on Apr 26, 2020 at 9:59pm PDT ‘’Baada ya kuona ujumbe ule waZari, nilimpigia simu  na kumueleza, licha ya tofauti zetu ila bado na mamheshimu sana.  Alienielewa na nadhani baada ya corona kuisha tutapanga namna ya kuwalea watoto wetu pamoja,’’ Diamond alisema. Inadaiwa kuwa ujumbe wa Zari ulikuwa umemtia wasiwawi Tanasha baada ya kupata habari kuwa Mondi hashughuliki katika kuwalea wanawe, Dona akiachiwa jukumu la kumlea mwanawe kivyake. Ujuembe wa Mondi kwa Zari huenda utampa tumaini tena.  
1
Aliomba taasisi mbalimbali zinazofanya biashara na Saccos hiyo, zipunguze urasimu katika utoaji wa uamuzi ili kuwawezesha wanachama kupata mikopo waliyoomba kwa wakati.Meneja huyo alisema ushirika huo ulianza mwaka 1990 ukiwa na wanachama 37 tu walioweka akiba ya Sh 129,600, wengi wao wakiwa ni watumishi wa ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa huo.Alisema sasa ushirika huo umefanikiwa kuongeza wanachama kufikia 697, wenye akiba za Sh 1,010,783,900, ambazo zinazunguka kama mtaji wa kukopeshana.Alisema hali hii imewezesha ushirika huo kuwa na baki ya mikopo kwa wanachama, yenye thamani ya zaidi ya Sh 1,735,609,883.Kuhusu thamani ya chama hicho tangu kianzishwe, Meneja huyo alisema imefikia Sh bilioni 5.8 kikiwa na hisa 41,655,000 , akiba Sh 951,611,670 na baki ya mikopo Sh 1,946,515,130.Akizungumzia kuhusu mikopo kutoka taasisi mbalimbali hapa mkoani, Meneja huyo wa Arusha Kurugenzi Saccos alisema mwaka wa 2013/2014 ushirika huo umepokea mkopo wenye thamani ya Sh bilioni moja kutoka Benki ya CRDB na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), ambapo NSSF imetoa mkopo wa Sh milioni 500.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Arusha Kurugenzi Saccos, Dk Freedom Makiago alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika ushirika huo kuwa wanachama wapatao 196 wamenufaika na mikopo yenye thamani ya Sh 621,576,000.
5
NA FLORENCE SANAWA – MTWARA   MWANAUME mmoja, Sharafi Issa, maarufu Zamda Salum (19), mkazi wa Kijiji cha Milango minne, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara kwa kosa la kujifanya mwanamke na kufunga ndoa na mwanaume mwenzake kisha kuishi naye nyumba moja kama mume na mke. Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo jana mbele ya Hakimu Mkazi Richard Kabate na kusomewa shtaka hilo na Wakili wa Serikali, George Makasi. Kabate alidai kuwa kitendo hicho cha watu wenye jinsia moja ya kiume kuishi nyumba moja kama mke na mume ni utovu wa kimaadili na ni kinyume na kifungu 157 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 sheria iliyofanyiwa marekebisho ya mwaka 2002. Alidai kuwa mshtakiwa Sharafi alitenda kosa hilo kwa nyakati tofauti mwezi Machi na Juni, mwaka huu katika vijiji vya Mkahala na Mpanyani ndani ya Halmashauri ya Mji wa Nanyamba mkoani Mtwara, kwamba kwa makusudi katika jamii, alijifanya mwanamke na kumshawishi Mustara Nurudin Saidi kwa kumtongoza na kufunga naye ndoa isiyo halali. Baada ya mshtakiwa huyo kusomewa shitaka hilo linalomkabili, alikana na Wakili Makasi aliiambia mahakama kuwa upelelezi bado haujakamilika.  
3
KATIKA mchezo wa jana, kati ya Simba na Yanga kulishuhudia matukio matano kabla ya mchezo huo kuanza, Yanga kugoma kuingia kushuka katika basi lao.-Yanga walifika Uwanja wa Taifa saa 9:25 alasiri, lakini wachezaji wao walikaa ndani ya gari kwa takriani dakika 20, huku baadhi ya makomandoo wakiwafukuza waandishi wa habari waliokuwa karibi na gari hilo. Ilikuwa tofauti kwa Simba, ambao wenyewe baada ya kufika uwanjani hapo walishuka katika gari lao na kuingia moja kwa moja katika chumba chao cha kubadilishia nguo.SIMBA WAIFUNIKA YANGAKishangiliaji au kuchangamka, Simba waliifunika Yanga kabisa kabla ya kuanza mchezo huo. Dakika 15 kabla ya kuanza kwa mchezo huo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu, mashabiki wa Simba walionekana kuwa wenye wenye furaha kubwa baada ya hamshahamsha yao kubwa iliyowafunika kabisa wenzao wa Yanga, ambao walionekana kama vile hawataki kabisa kelele baada ya kutulia vitini kimya, wakisubiri mtanange kuanza. Pamoja na hilo, kwa mtazamo tu ilionekana mashabiki wa Simba walijitokeza kwa wingi uwajani kushuhudia pambano hilo la watani wa jadi.VURUGU KWENYE MAGETIMashabiki wa pande zote mbili walionekana kuwa na usongo mkubwa wa kuingia ndani ya uwanja kushuhudia mpambano huo, walikutana na changamoto kubwa kutokana na idadi kubwa ya mashabiki waliotaka kuingia uwanjani kwa wakati mmoja, huku wasimamizi wa milangoni wakioneoneana kutojiandaa kupokea watu wengi kwa wakati mmoja.Baadhi ya mashabiki waliozungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kuwa, walikata tiketi lakini walizuiwa kuingia uwanjani baada ya mashabiki wa timu zote mbili kujaa uwanjani mapema na wengine kushindwa kupata sehemu ya kukaa, Wengine walikosa uvumilivu na kuamua kuondoka hata kabla mchezo haujaanza huku baadhi yao akilalamika wakidai mpangilio haukuwa mzuri na waliobaki wakijazana milangoni, walikutana na adha ya kufukuzwa na kutakiwa kukaa mbali kabisa.
4
WAKATI serikali ikiendelea na ujenzi wa reli ya kisasa kati ya Dar es Salaam na Mwanza yenye urefu wa kilometa 1,219 na pia kukarabati ile ya zamani maarufu kama `Reli ya Kati’, Shirika la Reli Tanzania (TRL), limetangaza kugeukia ujenzi wa reli za mijini, ikianza na Dar es Salaam na Dodoma.Lengo la reli hizo, limetajwa kuwa ni kuondoa msongamano katika maeneo ya mijini, lakini pia kuziunga sehemu zenye shughuli kuu za kiuchumi kama viwanda, ili kuweza kusafirisha bidhaa kwa urahisi.Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa alipokuwa anazungumzia mikakati mbalimbali ya kuimarisha usafiri wa reli nchini. Alisema kwa Dar es Salaam, mbali ya kuimarisha safari za sasa za ndani ya Dar es Salaam na maeneo jirani kama Pugu, zitajengwa pia reli mpya kati ya Mbezi na Bagamoyo, nyingine itakwenda Mbagala, lakini itakuwepo pia ya kwenda Uwanja wa Ndege.“Mpango huu wa kuwa na mtandao mpana wa reli za mijini unalenga kukabiliana na foleni, hasa ikizingatiwa katika miji na majiji kunakuwa na watu wengi, hivyo kukwamisha katika shughuli zao na foleni.“Ndiyo maana tunaangalia uwezekano wa kuwa na mtandao wa reli, tukianza na Dar es Salaam na Dodoma. Haya mambo yapo katika mipango kwa muda mrefu, ila kwa sasa tunakwenda kutenda. Ni suala la muda tu,” alisema Kadogosa ambaye ofisi yake inajiandaa kufyatua jingo la ghorofa saba eneo la Ihumwa, jirani na mji mkuu wa kiserikali wa Dodoma.Aliongeza kuwa reli hizo zitasaidia pia usafirishaji wa bidhaa kutoka viwandani, kwani zitakuwepo pia zitakazoungwa na viwanda ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na malighafi. Tayari Dar es Salaam kuna safari za treni za ndani ya jiji, ya Tazara- Pugu-Mwakanga, ya Stesheni ya Dar es Salaam-Pugu na Stesheni ya Dar es Salaam-Ubungo, ambazo zimetajwa kusaidia wakazi wake kutumia muda mfupi wa safari tofauti na mabasi ya abiria.Aidha, kwa kutumia usafiri wa treni, abiria wengi wamekuwa wakisafirishwa kwa wakati mmoja. Mathalani, kwa safari moja, treni kati ya Stesheni-Pugu husafirisha zaidi ya abiria 2,000 kutokana na mabehewa yake kati ya 19 na 23. Behewa moja hubeba abiria kati ya 80 na 120 na safari huchukua kati ya nusu saa na saa moja, wakati kwa safari kama hiyo kwa basi, abiria huweza kutumia hata saa 3-4.
3
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafi ri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imesema hakuna mgomo wa madereva wa mabasi yaendayo mikoani leo kama taarifa zilivyosambaa kwenye mitandao ya kijamii tangu Jumapili iliyopita.Hayo yalibainishwa jana Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Lameck Kamando kwenye mkutano wake na vyombo vya habari.Ujumbe huo ambao ulielezwa kusambazwa na Umoja wa Madereva uliwataka madereva wote wa mabasi kugoma kuanzia leo kwa nia ya kupinga adhabu za faini kubwa zinazotolewa na Sumatra kutokana na madereva hao kukiuka Mfumo wa Kudhibiti Mwenendo wa Mabasi (VTS) kwa kwenda mwendokasi wa zaidi ya kilometa 80 kwa saa.Kutokana na kusambaa kwa taarifa za mgomo huo ambao umeleta taharuki kwa wasafiri, Kamando alisema Sumatra ilikutana na wadau likiwemo Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA) na Chama cha Madereva Tanzania (UWAMATA) ambao kwa pamoja walisema taarifa hizo siyo za kweli, hivyo hakuna mgomo wowote.“Mgomo haupo kwa sababu ni batili na haukufuata kanuni na taratibu, kama kuna mtu anasisitiza upo basi ajitokeze na aeleze sababu za msingi za kuitisha mgomo huo, Sumatra tunawakumbusha wamiliki wa mabasi wafuate masharti ya leseni zao,” alisema Kamando.Kamando alisema kero za madereva hao wamezipokea na watazifanyia kazi. Mwanasheria Mkuu wa UWAMATA, Frank Sanga alisema licha ya mgomo huo kutokuwepo, lakini madereva wamekuwa na mgogoro wa muda mrefu na Sumatra kutokana na faini wanazotozwa kwa kutofuata kanuni za mamlaka hiyo badala ya Sheria ya Usalama Barabarani.Alisema hali hiyo imekuwa ikijitokeza zaidi mikoani hususani mkoani Morogoro ambako madereva hutozwa kati ya Sh milioni 1 hadi Sh milioni 28 na wakati mwingine hulazimishwa kulipa sehemu ya faini hizo hapohapo hali inayowafanya madereva kuyatelekeza magari na kukimbia.“Tumeshafungua kesi mbili Mahakama Kuu dhidi ya Sumatra, kesi namba 257/2019 na kesi namba 87/2019 ili mahakama itoe ufafanuzi kwamba madereva wanapaswa kuadhibiwa kwa sheria ya usalama barabarani au kwa kanuni ya Sumatra, kwa hiyo nawaomba madereva wasigome mpaka hapo mahakama itakapotoa maamuzi, kugoma wakati jambo liko mahakamani siyo sahihi, ni kuinyima haki mahakama kuamua kuhusu kile ambacho tumekipeleka mahakamani,” alisema Sanga.Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Fortunatus Musilimu, alisema baada ya kufuatilia ujumbe unaosisitiza kuwepo kwa mgomo huo, walibaini kuwa ulisambazwa na Umoja wa Madereva Tanzania lakini pasipo kuandikwa jina au cheo cha mhusika. Katika hali hiyo, alisema mgomo huo unakosa uhalali na ni kosa la jinai.
3
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza  hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi.  Kwa misingi kama hiyo sisi kama  chombo cha habari  tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk.  Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia.  Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”.  Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi,  Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii.  Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo.  Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge.  viongozi  wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo.
5
Katika kipindi cha kwanza Geita walionesha mchezo mzuri na kupata mabao yote katika kipindi hicho huku kipindi cha pili Polisi wakizinduka na kuishambulia Geita Gold Minning kwa kasi lakini mashambulizi hayo hayakuzaa matunda.Geita walianza kupata bao katika dakika ya 16 kupitia kwa winga wake Venance Joseph baada ya kupokea pasi kutoka ya Hussein kutoka magharibi mwa uwanja.Hata hivyo Polisi walijitahidi kufanya mashambulizi lakini kipa wa Geita Gold Minning Said Ally alikuwa makini kuokoa hatari langoni mwake.Geita walipata bao la pili kupitia kwa mchezaji yuleyule Joseph baada ya kuwazidi kasi mabeki wa Polisi Frank Sindato na Fidelis Sanja na kuuweka mpira kimiani.Polisi walifanya mabadiliko kwa kumtoa Faraji Mwinshehe na kumwingiza Ibrahim Mbogamasoli ambaye aliiongezea uhai timu hiyo.Katika kipindi cha pili Geita Gold Minning walifanya mabadiliko ya kumtoa Paul Michael na nafasi yake kuchukuliwa na Abubakary Mnyambegu lakini hawakuweza kubadili matokeo.Kutokana na matokeo hayo Polisi Dodoma imeendelea kubaki na Pointi 14, huku Geita Gold Minning ikijiongezea Pointi na kufikisha pointi 15.Mchezo unaofuata Polisi itakuwa ugenini kucheza na Toto Africans na Geita ikirudi nyumbani kucheza na JKT Kanembwa.
4
Na AVELINE KITOMARY-DAR ES SALAAM MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk. Yudas Ndugire, ametoa tahadhari kwa wakazi wa mkoa huo kuwa makini pindi wanapompokea mgeni anayetoka katika nchi zinazotajwa kuwa na ugonjwa wa ebola. Hatua hiyo imekuja mara baada ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Agosti 30 kuitaja Dar es Salaam kuwa mmoja wa mikoa iliyopo hatarini kwa ugonjwa huo. Akizungumza na MTANZANIA Jumapili, Dk. Ndugire alisema iwapo mkazi ataona dalili zozote, ni vema akatoa taarifa haraka katika mamlaka husika. “Ni kweli mkoa huu umetajwa kuwa kati ya mikoa nane iliyo hatarini na ebola, hii ni kutokana na Dar es Salaam kuwa mji mkuu wa kibiashara na una mwingiliano na watu kutoka katika nchi mbalimbali. “Hivyo lazima kila mtu awe makini, hasa pale anapompokea mgeni kutoka katika nchi zinazotajwa kuwa na ebola kama Uganda, Wilaya ya Kasese na Congo, unapoona ana dalili za kutoka damu sehemu mbalimbali, homa kali, kutapika, usimpime kwa mikono wala kumgusa, nenda katoe taarifa katika mamlaka husika,” alisema Dk. Ndugire. Alisema mkoa umeshaanza kuchukua tahadhari kwa kuunda timu ya uratibu ili ugonjwa usiingie pamoja na timu ya matibabu na vifaa. “Dar es Salaam haipo mpakani, lakini kuna uwanja wa ndege na pia stendi kubwa ya mabasi yanayotoka nje ya nchi, tumeunda timu ya uratibu ambayo kazi yao ni kuratibu timu nzima katika mapambano ya kuzuia ebola kuingia. “Sehemu kama airport wapo maofisa afya ambao wanafuatilia mienendo ya watu wanaotoka nje ya nchi, na hapo kuna vifaa maalumu vimefungwa vinavyohisi mgonjwa mwenye joto kali.  “Pia timu za matibabu zimeundwa kwa ngazi za manispaa na tayari wanapewa mafunzo, vilevile kuna jengo limeandaliwa katika Hospitali ya Temeke, kwa wagonjwa watakaohisiwa watapelekwa pale,” alieleza Dk. Ndugire. Alisema tayari wameshaanza kutoa elimu kwa wanachi kuhusu dalili za ugonjwa huo na namna ya kuuepuka.  “Elimu imeanza kutolewa kwa njia ya vipeperushi vyenye kuonyesha picha, hatua gani mwananchi anachukua akihisi kuna ugonjwa wa ebola, pia hata kwa njia ya vyombo vya habari tunatoa elimu,” alisisitiza Dk. Ndugire. Agosti 30, mwaka huu, Wizara ya Afya ilitaja mikoa ya Kigoma, Mwanza na Kagera kuwa katika hatari zaidi huku mikoa ya Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Dodoma na Dar es Salaam ikitakiwa kuchukua tahadhari zaidi. Shirika la Afya Duniani (WHO) Julai 17, mwaka huu lilitangaza kuwa mlipuko wa ebola ni janga linaloathiri afya ya jamii.
3
MAHAKAMA imeshauri ili kuondoa mrundikano magerezani, kesi zote ziwe na uwezekano wa mshitakiwa kupewa dhamana ikiwa ni pamoja na zile za mauaji na mshitakiwa aruhusiwe kujidhamini mwenyewe.Aidha imeshauri pia sheria zirekebishwe kusaidia kuondoa mrundikano magerezani kwa kupunguza adhabu ndefu. Akizungumza mara baada ya kuwaapisha mawakili 720 katika Chuo cha Sheria, Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma alisema utoaji wa adhabu kali za vifungo badala ya adhabu mbadala, makosa mengi kutokua na dhamana pamoja na ucheleweshaji katika upelelezi wa mashitaka ni mambo ambayo yanajaza watu magerezani na kwamba yanahitaji kupatiwa muarobaini.“Ukisikiliza mijadala bungeni kila mtu anataka adhabu kali, miaka 30, 15, hizo zote zinachangia magereza kujaa, na sisi mahakama tuna mapendekezo, kwanza tuwe kama Kenya makosa yote yapewe dhamana tuziachie mahakama, Kenya hata kesi za mauaji mahakama zinatoa dhamana,” alisema Jaji Mkuu.Alisema hivi karibuni walitembelea gereza la Butimba na kushuhudia hali ya msongamano wa watu gerezani na kukiri kuwa hayo ni mapungufu katika sheria na kuongeza kuwa Sheria zinaegemea katika adhabu kubwa katika kesi kama za mauaji, dawa za kulevya, uhujumu uchumi na ubakaji.Aidha, Jaji Mkuu alisema pia kuwa watu sasa wanatambulika kupitia vitambulisho vya taifa hivyo wanaweza kuruhusiwa kujidhamini. Alisema kuna kesi nyingine kama mkandarasi kukamilisha kazi, masuala ya mikataba wanakamatwa na kuwekwa mahabusu, alisema, “utasikia kamata, weka ndani, tuache masuala ya kijinai yaende kijinai na yanayohusu mikataba yaende kimikataba.”Aidha, Jaji Mkuu alisema upande wa mashitaka pia unachangia kuongeza watu magerezani kwa sababu wanakamata na kuwafungulia mashitaka watu kabla ya kukamilisha upelelezi.Alisema katika marekebisho ya sheria itamke kwamba ikipita muda fulani kabla upelelezi haujakamilika kesi ifutwe na sheria hiyo itamke pia kuwa mshitakiwa akifutiwa kesi asikamatwe na kushitakiwa tena kama inavyofanyika sasa.“Nadhani wa kulaumiwa ni wapelelezi na sio mtu mwingine na sababu wanazotoa mahakamani hazina mashiko, mwaka 2012 tangazo kilitolewa na DPP kwamba usikamate mtu kabla hujakamilisha upelelezi kwa bahati mbaya halifuatwi, watu wanakamatwa ndipo wanaenda kupeleleza. Sheria itamke tu mtu akiachiwa asikamatwe tena na Mahakama itatekeleza,” alisema Jaji Mkuu.Alisema ni Rais pekee mwenye uwezo wa kuwatoa watu magerezani bila amri ya mahakama kama ambavyo amekua akifanya katika msamaha unaotolewa katika sikukuu za kitaifa pamoja na msamaha alioutoa hivi karibuni. Akizungumzia mawakili waliapishwa, Jaji mkuu alisema kwa watumishi wa mahakama kwa sasa utaratibu ni tofauti, hawataweza kutoa huduma za kiwakili kwa sasa mpaka pale watakapoanza kazi hiyo.“Vitambulisho walivyopewa vinaonesha hawawezi kutoa huduma ya kiwakili kwa sasa hadi watakapoanzacha utumishi wa kimahakama, analinda namba yake tu ili wakistaafu wawe wabobezi katika uwakili, yule aliyeapishwa leo ana namba bora kuliko anayeapishwa kesho,” alisema Jaji Mkuu.Alisema kuwa kwa sasa vyuo vinazalisha mawakili wengi tofauti na awali na pia kuna wengine walisoma miaka mingi lakini walikua hawajakamilisha taratibu za kiwakili na kuamua kufanya sasa. Aliwataka pia wananchi kuwataja au kuwashitaki katika mamlaka husika watumishi wa mahakama wanaojihusisha na vitendo vya rushwa ili wachukuliwe hatua.
3
BUNGE limeazimia kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kutokana na kauli yake aliyodai kuwa Bunge ni dhaifu, kuwa ni ya dharau, kudhalilisha, kushusha heshima na hadhi ya Bunge.Mbali na CAG, pia Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amefungiwa kuhudhuria mikutano miwili (Mkutano wa 15 wa Bunge la Bajeti na Mkutano wa 16) kutokana na kutoa kauli ya kulidhaliliisha Bunge baada ya kuunga mkono kauli ya Profesa Assad ya kusema Bunge ni dhaifu. Azimio hilo la Bunge liliafiki jana baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kuiagiza Kamati ya Haki, Maadili, Kinga na Madaraka ya Bunge, kufanya uchunguzi kubaini kama CAG alihusika kusema kuwa Bunge ni dhaifu alipokuwa akihojiwa na chombo cha habari cha Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, Januari 9, mwaka huu.Kwenye mahojiano hayo mtangazaji alimhoji CAG: “Naona Ofisi ya CAG kwa upande wa Tanzania inafanya kazi nzuri sana ya kutoa ripoti kila mwaka zinazoonesha ubadhirifu wa fedha, lakini hawaoni hatua zinazofuata baada ya hapo...” Baada ya swali hilo, Profesa Assad alijibu kuwa: “ Kimsingi ni kazi ya Bunge, kama tunatoa ripoti kuna ubadhirifu lakini hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu wa Bunge.Bunge linatakiwa lisimamie na lihakikishe kuwa pale penye matatizo hatua zinachukuliwa, kazi yetu ni kuripoti tu na huo udhaifu ni jambo la kusikitisha. “Lakini tatizo kubwa nahisi Bunge linashindwa kufanya kazi yake inavyotakiwa, labda nasema jambo hili kwa sababu kunahusisha watu fulani lakini nafikiri Bunge likifanya kazi yake vizuri hata udhaifu unaoonekana....”Akiwasilisha taarifa ya shauri hilo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Emmanuel Mwakasaka, alisema baada ya kuagizwa na Spika, Profesa Assad alipewa wito kwa Mamlaka ya Bunge chini ya kifungu cha 15 na 16 cha Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge, Sura ya 296 ya kuamuru mtu yeyote kufika mbele ya Bunge au Kamati kutoa ushahidi kuhusu jambo lolote kama litakavyofafanuliwa katika hati ya wito. “Hati ya wito ilimtaka shahidi (CAG) kutoa maelezo ya kuhusika au kutohusika kwake kwenye tuhuma zinazomkabili na kama ikibainika aeleze kwanini asichukuliwe hatua kwa kukiuka kifungu cha 26(e) cha Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge.Mahojiano ya Bunge na CAG Mwakasaka alisema Januari 21 mwaka huu, CAG alifika mbele ya kamati ambapo alipohojiwa alithibitisha kuwa Januari tisa mwaka huu akiwa Marekani kupitia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ni kweli ndiye aliyetoa kauli zinazolalamikiwa. Alitaja sehemu ya maelezo hayo ya CAG: “ Ni kweli nilifanya mahojiano na UN Radio, New York Marekani. UN Radio ipo ndani ya makao makuu ya UN, ni chombo cha Umoja wa Mataifa ikiwemo Tanzania.Nilihojiwa na mtangazaji Arnold Kayanda aliniuliza swali ambalo mmelisikia au kulisoma na nililijibu kitaaluma...maneno yaliyotumiwa ni udhaifu wa Bunge. “CAG alisema maneno aliyoyatumia katika mahojiano “udhaifu wa Bunge” ni maneno ya kawaida kwani neno dhaifu ni neno la kawaida katika lugha ya ukaguzi wa hesabu na hakuwa na nia ya kudharau Bunge bali tatizo lililopo ni tofauti ya tafsiri ya maneno aliyotumia.Aliendelea kumnukuu CAG: “Majibu yangu katika mahojiano....hayakuwa na nia ya kudhalilisha Bunge hata kidogo....Katika lugha ya kikaguzi udhaifu huja kwa namna mbili, kwanza ni katika tathimini za taasisi na mifumo na pili ni katika kukazia hoja kuonesha kiwango cha mapungufu ndani ya taasisi moja. Mwakasaka alisema CAG alipohojiwa kuhusu maana ya maneno “udhaifu” kwa wananchi wa kawaida na watu ambao taaluma yao si wahasibu wa wakaguzi, alijitetea kuwa alikuwa na maana ya upungufu na si vinginevyo.Alisema alipooneshwa tafsiri ya neno dhaifu kama lilivyotafsiriwa na kamusi ya Kiswahili, ilionesha kuwa dhaifu ni goigoi au gonjwa, alionesha kutounga mkono tafsiri ya kamusi. Aidha, alieleza kutokana na ushahidi wa CAG wa kukiri kutoa kauli zinazolalamikiwa jambo lililothibitishwa na ushahidi wa video iliyosambaa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, vilivyomuonesha Profesa Assad akihojiwa. Tafsiri ya neno dhaifu Mwakasaka alisema neno dhaifu ni dhahiri lililenga kulishushia hadhi Bunge na hivyo kulidharau na kulidhalilisha Bunge mbele ya umma na duniani hasa ukuzingatia neno hilo lina dhana hasi.Alisema utetezi wa CAG kuwa hakumaanisha udhaifu wa Bunge hauna mashiko kwani maana ya neno dhaifu haibadili udhalilishaji kwani huleta hadhi hasi ya kitu kilichozungumzwa. “Mazingira aliyotumia neno dhaifu hayakuwa katika kutekeleza kazi za kihasibu au kikaguzi bali aliongea na ulimwengu mzima ambao si wote ni wahasibu au wakaguzi.” “ Pia kamati iliridhika kuwa shahidi (CAG) hakutoa angalizo lolote kuwa anazungumza katika tafsiri za kihasibu ili kuzuia tafsiri ya kawaida ya lugha. “Akiwa kwenye kamati CAG alikiri kuwa maneno aliyoyatumia yameleta tafrani na malumbano makali hasa kwenye magazeti na mitandao mbalimbali ya kijamii.“Kamati iliona kuwa ujumbe uliotolewa haukuwalenga wakaguzi wala wahasibu bali yeyote aliyemsikiliza. Kushindwa kwake kuchukua tahadhari kunadhihirisha kuwa alidhamiria kufanya kitendo hicho chenye kudharau na kudhalilisha Bunge na shughuli zake. Aidha, alisema utetezi wa CAG unaendelea kukosa nguvu kwa maelezo yake hasa kamati ilipotaka kujua kama ipo kanuni au mwongozo wa matumizi ya maneno rasmi ya kikaguzi na kihasibu inayoonesha neno dhaifu kuwa ni neno la kawaida. “CAG alijibu kuwa hakuna mahali palipoandikwa tafsiri hizo.Aliulizwa pia kama amewahi kuiita ofisi yake kuwa dhaifu kwa kuwa ni neno la kawaida, pia alikana kuwa hajawahi. “Pamoja na shahidi kukiri neno dhaifu alilolitumia halikupokewa vema na umma lakini hakuwa tayari kukiri kukosea au kutumia neno hilo lenye kudhalilisha. Mwakasaka alisema Kamati inaona CAG alikusudia kufanya udhalilishaji na alikuwa na nia ovu na Bunge kwa kuwa, alipohojiwa aliithibitishia kamati kwamba aliyapima maneno aliyoyatumia kabla ya kufanya mahojiano husika na alijiridhisha kuwa yote ni sahihi, hivyo ni wazi hata athari zilizojitokeza alizijua.Alisema pia Kamati imejiridhisha pasipo shaka kuwa CAG hakuwahi kujutia kauli yake akiwa mbele ya kamati au nje ya kamati na hakua tayari kuoana kitendo alichofanya kina dosari. Akizungumza na Habari- Leo kwa njia ya simu, Katibu wa Bunge Stephen Kagaigai alisema suala la uwasilishwaji wa taarifa ya CAG bungeni halitaathiriwa na uamuzi wa Bunge kutokana na taarifa hizo kusomwa na Waziri wa Fedha na Mipango.“Anayesoma taarifa bungeni ni Waziri wa Fedha na Mipango, hivyo uamuzi wa Bunge hautaathiri usomwaji wa taarifa ya CAG kama taarifa hizo zitawasilishwa bungeni ingawa mpaka sasa taarifa ya CAG haijatufikia,” alisema. Kibano kwa Mdee Mdee alikuwa anakabiliwa na tuhuma za kulidharau na kulidhalilisha Bunge kutokana na kauli yake ya Januari 2, mwaka huu aliponukuliwa na kusikika kwenye mitandao ya jamii akipongeza kauli za Profesa Assad kwamba Bunge ni dhaifu.Mwakasaka alinukuu kauli ya Mdee akisema: “Kitendo cha CAG kusema kwamba hali si nzuri halafu chombo kinachotakiwa kusimamia hali hakifanyi hivyo, ni cha kijasiri na nina imani wanaoongoza huo mhimili watakuwa wavumilivu”. Mwakasaka alisema akiwa mbele ya kamati, Mdee alikiri wazi kutamka maneno hayo, lakini alitoa maana ya neno udhaifu kwa mujibu wa Kamusi Kuu ya Kiswahili kuwa ni “hali ya kukosa nguvu kimaumbile, kifedha, kiuwezo na kiutendaji”.Alisema Kamati ilifanya utafiti kwa kuangalia maana ya neno ‘dhaifu’ katika Kamusi Kuu ya Kiswahili iliyoidhinishwa na Baraza la Kiswahili Tanzania na Baraza la Kiswahili la Taifa Kenya (KICD) na ilionesha dhana hasi. Alisema Mdee aliiambia kamati kuwa aliunga mkono kauli ya CAG Assad kwa kuwa ni haki yake kikatiba, lakini akakiri kukosea kutumia neno ‘udhaifu’ dhidi ya Bunge baada ya kuelezwa maana yake kwa mujibu wa kamusi. Mwakasaka alisema baada ya mahojiano Kamati iliona alikuwa na dhamira ovu ya kulidharau na kulidhalilisha Bunge mbele ya umma na kuwa Kamati imependekeza kumfungia kushiriki mikutano miwili, mapendekezo ambayo yaliungwa mkono.Lema kiaangoni Kabla ya Bunge kuridhia pendekezo la Bunge kumfungia Mdee, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) wakati akichangia hoja, alinukuu maneno yaliyotumiwa na Mdee na kisha akaunga mkono kuwa Bunge ni dhaifu. Lema alisema: “Roho ya mwenendo wa nchi inategemea uimara wa Bunge, sasa amesema Bunge ni dhaifu, ni kweli, na mimi kama mbunge wa vipindi vitatu nathibitisha hilo.Mheshimiwa, na mimi mbunge wa vipindi viwili, nathibitisha Bunge hili ni dhaifu”. Kutokana na kauli hiyo, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson, aliyekuwa anaongoza mjadala huo, alimtaka Lema kufika mbele ya Kamati hiyo. Matakwa ya kikatiba ya ripoti ya CAG bungeni Ripoti ya CAG huwasilishwa bungeni ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 143(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005.Ibara ya 144 (2) ya Katiba inasema CAG aweza kuondolewa katika mamlaka ya kazi yake kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake (ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote) au kwa sababu ya tabia mbaya, au kwa kuvunja masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, na hataweza kuondolewa kazini ila kwa masharti ya Ibara ndogo ya [4] ya ibara hii.
3
Aveline Kitomary – Dar es Salaam WANAWAKE wenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi (VVU) sasa wana uwezo wa kupandikizwa mimba na hatimaye mtoto kuzaliwa bila kuwa na maambukizi hayo. Hayo yameelezwa na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Vicent Tarimo katika mahojiano maalumu na MTANZANIA. Katika mahojiano hayo yaliyofanyika Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki hii, Dk. Tarimo alisema kuwa upandikizaji mimba watakaofanya ni mtu kupandikizwa yai lake mwenyewe, hivyo hata wagonjwa wa VVU wataweza kupandikizwa mimba na mtoto atazaliwa akiwa salama kabisa. Alisema kutokana na upandikizaji huo, hatua hiyo itakuwa ni njia salama isiyoruhusu maambukizi na mtoto atakayetungwa katika mimba hiyo atakuwa salama kwa kuwa maambukizi ya VVU kwa mtoto kipindi akiwa tumboni inakuwa asilimia ndogo. “Mama mwenye VVU ana uwezo wa kumzaa mtoto ambaye hana maambukizi kwa asilimia 45 bila kutumia dawa yoyote, kwani mwili unamkinga mtoto asipate maambukizi. “Hivyo VVU haizuii upandikizaji wa mimba, na hata kwa wale wenye magonjwa mengine tutashauriwa na daktari wa ugonjwa husika ili tuweze kuona kama hali ya mgonjwa inaruhusu kupandikizwa miamba au la,” alisema Dk. Tarimo. Kwa mujibu wa daktari huyo, kigezo cha kwanza kwa upandikizaji mimba ni lazima wahusika wawe wanandoa, kwa kuwa hiyo ndiyo njia rahisi zaidi kwa sasa, hasa kwa kuepuka migogoro. Alisema katika hilo, ili kuweka mazingira mazuri, kabla ya kuanza kutoa huduma ya upandikizaji mimba, taratibu na sheria zitatungwa kulingana na tamaduni ili kuepusha migogoro. “Sisi tuna taratibu na tamaduni, hivyo sheria itapangwa na wadau wa afya ili kuepusha migogoro baada ya upandikizaji mimba, ili kuweza kukabiliana na changamoto hizo, taratibu ziwekwe, lazima sheria ya upandikizaji mimba iwepo kabla ya kuanza upandikizaji,” alisema Dk. Tarimo. Alieleza kuwa uhitaji wa huduma ya upandikizaji mimba ni mkubwa nchini ambapo katika kliniki yake ya siku moja anawaona wahitaji saba hadi nane. “Wapo watu wengi tu wanaotamani huduma hii ianze kutolewa, hivyo kuna uhitaji mkubwa zaidi, hasa kwa wanandoa ambao wanahudhuria kwenye kliniki,” alisema Dk. Tarimo. Hata hivyo alisema gharama za huduma hiyo ni kubwa kutokana na uhalisia wa gharama za afya kuwa za bei ghali. “Kiuhalisia huduma za afya ni gharama sana, ndiyo maana hata Serikali inasisitiza matumizi ya bima kwa watu wote ili kupunguza mzigo wa gharama zinazotokana na msamaha,” alibainisha Dk. Tarimo.
3
Na MWANDISHI WETU -MOROGORO ANNA  Mayunga ambaye ni mama mzazi wa wakili maarufu, Peter Kibatala amefariki duniani baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba yake. Akiongea na MTANZANIA jana kwa njia ya simu, Wakili Kibatala alisema mama yake alifikwa na umauti wakati akikagua eneo la nyumba yake iliyoko eneo Fokoland, SUA mjini Morogoro. “Baada ya mvua ilinyesha leo (jana) asubuhi saa mbili aliamua kukagua nyumba kwa kuizunguka ili kuona kama maeneo yetu yamepata madhara, ghalfla ukuta wa nyumba ulianguka na kupoteza uhai wa mama,” alisema Kibatala kwa ufupi Taarifa zaidi zilizopatikana kutoka Morogoro zilieleza kuwa mvua hizo zilibomoa  nyumba kadhaa huku nyingine zikizingirwa na maji katika maeneo ya Kata ya Mafisa na Kihonda zilizo katika Manispaa ya Morogoro. Ilielezwa kuwa mvua hizo zilisababisha adha ikiwamo kuziba njia kadhaa mkoani humo pamoja na mafuriko na hivyo baadhi ya wanafunzi walishindwa kwenda shule. Baadhi ya wakazi maeneo mbalimbali ya mkoani humo walieleza kuwa mafuriko hayo yaliyakumba zaidi maeneo ya Kichangani, Mazimbu, Chamwino, Mbuyuni, Kilakala, Boma na sabasaba. “Mvua imesababisha shughuli za biashara na hasa maduka katikati ya Manispaa kufungwa  baada ya maji kuingia ndani na kusababisha uharibifu wa bidhaa mbalimbali. “Madhara mengine ni kuharibika kwa miundombinu ya barabara baada ya kujaa maji. Wananchi walilazimika kuvushwa kwa kubebwa mgongoni kwa Sh1,000 Diwani wa Kata ya Mafisa, Daud Salumu (CCM), alisema nyumba mbili zilizo kwenye kata yake zimebomoka  na nyingine zimezingirwa na maji. Alisema kila mwaka kata yake inakumbwa na mafuriko hivyo ipo haja kwa halmashauri  kuangalia namna ya kuepuka mafuriko hayo. Akizungumzia hali hiyo, Mhandisi wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (Tarura), Mkoa wa Morogoro,  Lusingi Mashashi alisema wanashirikiana na halmashauri ya manispaa ya Morogoro kuhakikisha miundombinu yote ya barabara inarekebishwa kwa wakati. Naye Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Inspekta Shomary Sala alisema eneo la Kihonda polisi walimuokoa mwanafunzi aliyekuwa amesombwa na maji wakati akivuka mto.
3
  Na MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM KAMPUNI ya simu ya Tigo imezindua huduma mpya ya kidigitali inayoitwa Twende App ambayo ni suluhisho la kuita teksi na kuwapatia wateja wake huduma sahihi na wanayoimudu nchini. Kwa kuunganishwa moja kwa moja na madereva wa teksi, huduma hiyo inawawezesha watumiaji kufurahia kiwango cha chini kuliko ambavyo wangetumia njia nyingine mbadala za mitaani. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Huduma za Kidijitali wa Tigo, Tawonga Mpore, alisema huduma hiyo ni kielelezo cha Tigo kujikita katika mageuzi ya mtindo wa maisha ya kidijitali kwa kutoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili wateja wake. “Tunaamini kuwa Twende App itatoa huduma nzuri kwa abiria kwa kuwaunganisha  na madereva ambapo watapata huduma bora na za gharama nafuu,” alisema. Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. Hassan Mshinda ambaye aliishukuru Tigo kwa kubuni mbinu nzuri zitakazowasaidia vijana kumudu maisha na kwamba amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wajasiriamali vijana wanapata msaada muhimu katika teknolojia ya kisasa. Alisema katika kufikisha malengo yao na kwa huduma hiyo, anaamini itawapatia fursa mpya zenye manufaa kwa madereva wote jijini Dar es Salaam. Naye Ofisa Mtendaji na Mwasisi wa Twende App, Justin Kashaigili, alisema amesukumwa na kasi ya maendeleo ya mbinu na nguvu ya ujasiriamali nchini. “Ninatarajia kuwapatia wakazi wa Dar es Salaam chaguo wanalolimudu, rahisi na linalofaa kwa ajili ya usafiri salama,” alisema. Alisema ili kujiunga na huduma hiyo, abiria anatakiwa kupakua Twende App katika simu yake ambayo itamuunganisha na dereva moja kwa moja badala ya kuhangaika kwenda mwenyewe kufuata sehemu ilipo teksi.
3
Na ASHA BANI SERIKALI imetangaza kushusha bei ya dawa na vifaa tiba hapa nchini, baada ya kuanza kufanya ununuzi wa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji wa ndani na nje ya nchi bila kutumia mawakala. Punguzo hilo limehusisha mikataba na wazalishaji 73, kati yao 10 ni wazalishaji wa ndani na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) inaagiza dawa, vifaa vya maabara na vitendanishi kutoka nchi 20 tu. Akitangaza mabadiliko hayo Dar es Salaam jana, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema kushuka kwa dawa hizo ni agizo la Rais Dk. John Magufuli. “Hatua ya kununua dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji kama tulivyoeleza hapo awali imesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za kununua dawa kwa asilimia 15 hadi 80. “Mabadiliko haya ya bei, yaani unafuu huo wa bei kiuhalisia umeanza kuonekana tangu Julai Mosi, mwaka huu ambapo wazalishaji wanaleta dawa MSD. Kupungua kwa bei kutaviwezesha vituo vya afya na hospitali kununua dawa zaidi kwa bei nafuu,” alisema Ummy. Alizitaja baadhi ya nchi walizotoa vibali kwa wazalishaji 46 ni Uganda, Denmark, Ufaransa, Ujerumani, China, Afrika Kusini, Falme za Kirabu, Bangladeshi, India, Tanzania na Kenya. Alisema aina 178 za dawa zinatoka kwa wazalishaji hao, huku vifaa tiba, jumla ya wazalishaji 18 wamepata mikataba kutoka katika nchi ya Uingereza, Ujerumani, India, Kenya na Tanzania. Alizitaja baadhi ya dawa hizo kuwa ni chanjo ya homa ya ini iliyouzwa kwa Sh 22,000 kwa sasa itauzwa Sh 5,300, dawa ya sindano ya diclofenac kwa ajili ya maumivu vichupa 10 vya dozi, awali ilikuwa ni Sh 2,000, sasa itauzwa kwa Sh 800. Pia alisema shuka moja iliyokuwa ikiuzwa kwa Sh 22,000, sasa itauzwa kwa Sh 11,000, mipira ya kuvaa mikononi inayokaa 50 kwa boksi itakuwa ikiuzwa Sh 18,200 kutoka Sh 19,200 na dawa ya kupambana na maambukizi ya bakteria yenye vidonge 15 itauzwa Sh 4,000 kutoka Sh 9,800. Pia amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri, waganga wakuu wa wilaya na mikoa kuhakikisha bei ya dawa zinashushwa kama watakavyoelekezwa na MSD. Alizitaka halmashauri, vituo, hospitali kutumia bei elekezi ya dawa iliyotolewa na wizara hiyo iliyopo katika kitabu cha MSD. Alisema watakuwa wanabandika mabango kama wanavyofanya Ewura na ikitokea muuzaji hajatekeleza hatua za kisheria zitachukuliwa mara moja. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu, alisema watajitahidi kuhakikisha dawa zinapatikana kwa asilimia 100, huku akimwomba Ummy kuhakikisha halmashauri na hospitali zinawasilisha mahitaji yao kwa wakati. “Tunaomba ushirikiano wa wadau wote, tumejipanga kuhakikisha tunavuka malengo kusambaza dawa kutoka asilimia 81 ya sasa hadi 100,” alisema. Pia alisema MSD itahakikisha dawa zinapatikana kwa wakati, hivyo ni muhimu wananchi kutoa ushirikiano.
3
Mohamed Hamad, Kiteto Barabara ya km 88.4 iliyogharimu zaidi ya Sh bilioni sita kutoka Kata ya Nameleck, Lortepesi na Sunya, imeharibika vibaya na mifugo wakiwamo ng’ombe na punda wanaochungwa barabarani na wafugaji. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Tamimu Kambona amesema, barabara hiyo iliwekwa alama zote za barabarani lakini zimeng’olewa ambapo hata katika maeneo ya vivuko vya mifugo, ng’ombe hawapiti na  badala yake mifugo hiyo imekuwa ikitembezwa barabarani kama magari. “Miundombinu ya barabara imeharibiwa ikiwamo ya Kibaya Ndedo, Kibaya Kijungu na maeneo mengine kama Lengatei na Sunya kuna uharibifu mkubwa ikiwamo mifugo kutembezwa barabarani ikizingatiwa Serikali imetumia gharama kubwa,” amesema. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Ndedo, Paulo Laiza akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kata yake amesema, kila mara mifugo imeendelea kugongwa katika eneo lake na kusababisha umaskini kwa wananchi hao na kuomba Serikali kuingilia kati. “Mwenyekiti naomba Serikali itusaidie eneo langu la Ndedo ni juzi tu ng’ombe 24 waligongwa barabarani na kila mara nimekuwa nikilalamika hapa mifugo kugongwa cha ajabu mwenye mifugo tena ndiyo anayetakiwa kulipa gari, huu unyanyasaji utaendelea hadi lini,” amehoji Laiza. Aidha, Diwani wa Kata ya Partimbo, Paulo Tunyoni ameiomba Serikali kuelimisha wafugaji kutotembeza mifugo hiyo barabarani sanjari na kuwekwa alama za barabarani, maeneo ya kuvukia mifugo. Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto na Diwani wa Kata ya Chapakazi, Lairumbe Mollel, amesema kwenye kikao cha madiwani cha taarifa za robo ya kwanza ya mwaka kuwa sheria zilizopo mfugo mmoja akikamatwa anatakiwa kutozwa faini ya Sh 5,000. “Waheshimiwa madiwani tulipitisha sheria, jukumu letu ni kuelimisha watu wetu ili kupunguza madhara, ikumbukwe hili suala la mifugo kugongwa barabarani ni kila mara, cha kusisitiza hapa tengenezeni maeneo ya mapalio ya kupitisha mifugo,” amesema.
3
Na MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM UPINZANI unaoonyeshwa na klabu kongwe nchini, Simba na Yanga, umeonyesha kumvutia mchezaji wa kimataifa wa Kenya, anayechezea klabu ya Tottenham Hotspurs, kiungo mkabaji Victor Wanyama. Simba na Yanga ni wapinzani wa jadi nchini, ambapo upinzani wao umekuwa ukikua siku hadi siku, hali inayofanya mchezo kati ya timu hizo mbili kuingia katika rekodi ya mapambano bora Afrika. Ukiacha pambano kati ya timu za Super Sports na Mamelody Sundown za Afrika Kusini, Hearts of Oak na Asante Kotoko ya Ghana, hutaacha kuzungumzia pambalo lingine bora ambalo linakutanisha timu hizi za Simba na Yanga na kuvuta hisia za mashabiki wengi. Wanyama yupo nchini kwa ajili ya mapumziko, baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu nchini England, ambapo ameambatana na wadogo zake. Akizungumza na MTANZANIA jana, Wanyama alisema timu hizo zimekuwa zikimvutia kutokana na upinzani wao unaoleta tija katika soka la Tanzania. “Atakayekwambia hazijui klabu za Simba na Yanga atakuwa anakosa raha sana, navutiwa na upinzani wao, ambao kwa hakika unalitangaza soka la Tanzania. “Huwezi kulitaja soka la Tanzania bila kutaja klabu hizo, zinajulikana na nina imani hata baadhi ya watu na timu kubwa barani Ulaya zinasikia kuhusu hizi timu,” alisema Wanyama. Lakini Wanyama alieleza kuwa, kabla ya kupata nafasi kucheza soka la kulipwa Ulaya, hakuwahi kufikiria kucheza katika klabu hizo, isipokuwa Azam. “Sikuwahi kufikiria kucheza katika klabu hizo, licha ya umaarufu wake, ila Azam niliwahi kuifikiria na hii ni kutokana na urafiki wangu na Yusuph Bakhresa,” alisema. MTANZANIA lilimpata Yusuph, ambaye naye alieleza kuwa, kama klabu wangefarijika kama Wanyama angeamua kutua katika klabu hiyo, kwani ni mchezaji mkubwa. “Ingekuwa faraja kubwa kwetu kama Wanyama angecheza Azam na mafanikio yake angeanzia kuyapata akiwa na timu yetu, hakuna klabu ambayo haitamani kuwa na mchezaji kama yeye, ila tunamkaribisha wakati mwingine akiona inafaa kucheza Azam,” alisema Yusuph. Akizungumzia soka la Tanzania, Wanyama alisema linazidi kupiga hatua, japo kuna nguvu ya ziada inahitajika kuweza kulisukuma kufikia mafanikio makubwa. Hata hivyo, mchezaji huyo jana alikuwa mmoja kati ya watu walioshuhudia mchezo wa Ndondo Cup kati ya Kauzu FC na Faru Jeuri, katika Uwanja wa Kinesi, michuano ambayo imekuwa gumzo nchini kutokana na kuibua vipaji. Kabla ya kushuhudia mchezo huo, Wanyama alisema anavutiwa na michuano ya aina hiyo, kwani inatoa fursa kwa wachezaji kuonyesha uwezo wao, hasa wale wasiokuwa na timu zinazoshiriki Ligi. Wanyama aliwahi kucheza klabu za Nairobi City Star, AFC Leopards Helsingborg zote za nchini Kenya, Baada ya hapo, nyota huyo alicheza ligi ya Ubelgiji akiwa na timu ya Beerschot, kabla ya kuhamia Celtic, Southampton na Tottenham, zote za Ligi ya Uingereza.
4
Na SAFINA SARWATT-SIHA KATIBU wa Itikadi na Uenzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Humphrey Polepole, amesema chama chake kitaielekeza Serikali iwatafutie wananchi wa Kata ya Eldrument, ekari 4000 kwa ajili ya ujenzi wa makazi baada ya CCM kushinda ubunge wa Jimbo la Siha, Mkoa wa Kilimanjaro. Polepole aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa kampeni katika Kijiji cha Matandi, Kata ya Eldrument, alipokuwa akimnadi mgombea Ubunge wa CCM, Dk. Godwin Mollel. “Kama CCM tutashinda ubunge wa jimbo hili, tutaielekeza Serikali itafute ekari 4000 kwa ajili ya  wananchi wa Kata hii ya Eldrument ili mkajenge makazi yenu ya kudumu. “Pamoja na hayo, tukishinda mjue tutamalizia ujenzi wa Zahanati ya Sinai iliyoko Kata ya Ormelili kwa sababu CCM ndiyo chama kikubwa kinachoongozwa kwa ilani inayotekelezeka,” alisema Polepole. Kwa upande wake, Mgombea Ubunge, Dk. Mollel, alisema vyama vya upinzani ni sawa na kikundi cha Saccos na havina uwezo wa kuongoza nchi. “Namshangaa Mbowe kwa kauli zake, kwamba mimi ni sawa na gunia la misumari na sibebeki. Najua aliyasema hayo kwa sababu anajua mimi siwezi kuingia kwenye vita ya kitoto. “Kwa hiyo, nawaombeni ndugu zangu, mchague gunia la misumari ili tukajenge nchi. Najua Chadema wamenitukana sana, lakini siogopi matusi kwani kiu yangu kubwa ni maendeleo ya wananchi na si kufungwa mdomo kwa namna yoyote. “Mkinipa kura, nitashughulika na kero zenu bila kujali chama kwani nipo kwa ajili ya masilahi ya watu wa Siha,” alisema Dk. Mollel. Wakati huo huo, mgombea ubunge kupitia Chama cha Sauti ya Umma (SAU), Mdoe Azaria, alisema kama atafanikiwa kushinda ubunge wa jimbo hilo, atatoa nusu ya mshahara wake kwenda katika halmashauri ili fedha hizo zitumike kutatua kero za wananchi. Katika hatua nyingine, Mgombea Ubunge Jimbo la Siha kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Tumsifuel Mwanri, alisema endapo wananchi wa Siha watamchagua, atahakikisha anatatua kero za elimu, maji, afya na migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji. Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni jana, Masoud Omar ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CUF Taifa, aliwataka wananchi kuchagua watu wasiofunga plasta ili wakawaletee maendeleo. Kwa upande wake, Mgombea wa Chadema, Elvis Mosi, aliwataka wananchi wa jimbo hilo kujitokeza na kumpigia kura siku ya uchaguzi Februari 17, mwaka huu  na kuachana na maneno yanatolewa na baadhi ya watu kuwa hali ya usalama si shwari jimboni humo. “Ndugu zangu wana-Siha, suala na ulinzi na usalama naamini limeimarishwa na Jeshi  la Polisi, kila mmoja ahakikishe kuwa anatumia haki  yake  vizuri ya kupiga kura na kumpa kiongozi atakayeweza kuwaletea maendeleo,” alisema Mosi.
3
London, England BINGWA wa mbio za magari kutoka nchini England, Lewis Hamilton, ameshinda ubingwa wa michuano ya British Grand Prix baada ya kumshinda mpinzani wake, Nico Rosberg, huku wote wakitumia gari aina ya Mercedes. Huu ni ushindi wa tatu mfululizo kwa Hamilton katika mashindano ya nyumbani nchini England. Katika ushindi huo, Hamilton alitumia saa 1: 34 na sekunde 55, wakati mpinzani wake Rosberg akitumia saa 1:35 na sekunde 12. Hata hivyo, Hamilton amedai kwamba hakuwa na uhakika wa kushinda kutokana na upinzani aliokutana nao katika michuano hiyo, ila amempa pongezi mpinzani wake kwa changamoto alizompa. “Sidhani kama kuna mtu anaweza kuwa na furaha kama nilionayo, ukweli ni kwamba nina furaha ya hali ya juu, hii inamaanisha kwamba  British Grand Prix ni michuano bora kwetu. “Nilikuwa na upinzani mkubwa nikawa na wasiwasi, lakini nashukuru ninazidi kutetea ubingwa wa michuano hii, nilikuwa ninauelewa uwezo wa Rosberg, hivyo nilikuwa na wakati mgumu wa kushinda kutokana na hali ya hewa. “Mvua iliyokuwa inaendelea ilianza kunipa shida, ila niliweza kupambana hadi hatua ya mwisho,” alisema Hamilton. Inadaiwa kuwa Hamilton ni miongoni mwa madereva 22 duniani wenye mvuto na idadi kubwa ya mashabiki, baada ya kushinda taji hilo mashabiki walijitokeza kwa wingi wakishangilia kwa kumwinua juu.
4
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman ameitaka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kurekebisha sheria zilizopitwa na wakati ambazo baadhi hazifanyi kazi tena.Suleiman alisema hayo wakati akiagana na wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Mazizini kutokana na kutenganishwa kwa wizara na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu.Alisema katika kipindi cha miaka mitatu, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ilifanya kazi kubwa ya kuzifanyia marekebisho sheria zilizopitwa na wakati. Alizitaja sheria zilizofanyiwa marekebisho katika kipindi chake ni pamoja na sheria ya ushahidi ambayo ilikuwa ikilalamikiwa kwa muda mrefu.“Mafanikio yangu makubwa katika kipindi cha miaka mitatu nilipokuwa Waziri wa Katiba na Sheria ni kufanyiwa marekebisho kwa sheria ya ushahidi ambapo sasa ushahidi wa mtoto unatambuliwa,” alisema.Aliyataja marekebisho mengine yaliyofanyika katika sheria zilionekana kikwazo katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia ni Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2017.Alisema sheria hizo kwa kiasi kikubwa zimeleta mabadiliko makubwa na kudhibiti matukio ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia na kutambua ushahidi unaotolewa na mtoto ambaye hajafikia umri wa miaka 18.“Naipongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kwa kazi kubwa ya kuzifanyia marekebisho sheria zilizopitwa na wakati ambazo ni kikwazo katika kutekeleza majukumu ya wananchi,” alisema.Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hassan Said Mzee alisema wataendelea kuzifanyia marekebisho sheria zilizopitwa na wakati ambazo hazina maslahi kwa jamii.“Ofisi ya Mwanasheria Mkuu moja ya vipaumbele vyetu ni kuzifanyia marekebisho sheria zilizopitwa na wakati ambazo hazina tija kwa jamii,” alisema.Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria, Jaji Bakari Mshibe alisema zipo sheria ambazo zinahitaji marekebisho makubwa zikiwa na lengo la kuleta mabadiliko ya sheria.“Miongoni mwa kazi tunazotarajiwa kuzifanya ni kurekebisha sheria zilizopitwa na wakati na kutunga mpya ili kuleta mabadiliko makubwa ya wakati uliopo,” alisema.
3
Kulwa Mzee, Dar es Salaam Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera (39), ambaye hali yake ya kiafya bado ni tete, arudi mahakamani baada ya siku saba ili kupata taarifa ya matibabu. Uamuzi huo ulitolewa leo saa tatu asubuhi wakati kesi hiyo ilipokuwa ikitajwa katika mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile. Mahakama ilimpa nafasi Kabendera kuelezea maumivu anayosikia ambapo akijieleza alidai hali ya kushindwa kupumua usiku bado inaendelea na siku nane zilizopita alisikia maumivu makali mguu wa kulia, maumivu makali katika mfupa ndani ya paja hali inayomfanya akose usingizi. Anadai alionana na daktari jana akamwambia kulikuwa na ugeni anamsikiliza kesho lakini mara ya mwisho aliomuona Alhamisi iliyopita na tiba aliyopata ni kupimwa damu na kuchomwa sindano tatu za maumivu. Baada ya maelezo hayo, Hakimu aliamuru arudi Septemba 18 ili aje kueleza kitu gani alichofanyiwa baada ya kuonana na daktari. Awali, Wakili wa Kabendera, Jebra Kambole aliendelea kusisitiza kwamba afya ya mteja wake inaendelea kutetereka, mguu wa kulia umepooza na hajapata tiba sahihi wanaomba apelekwe katika hospitali za Serikali ili afanyiwe vipimo. Upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika. Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Kabendera anakabiliwa na na mashtaka matatu ambapo shtaka la kwanza ni kwamba kati ya Januari mwaka 2015 na Julai 2019 maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam Kabendera na wengine ambao hawapo mahakamani anadaiwa alitoa msaada kwenye genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia fedha. Inadaiwa shtaka la pili, mshtakiwa anadaiwa kukwepa kodi, inadaiwa kati ya Januari, 2015 na Julai 2019 maeneo mbalimbali ya DAR es Salaam bila sababu za msingi alikwepa kulipa kodi Sh 173,247,047.02 kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Katika shtaka la tatu la kutakatisha fedha, inadaiwa katika tarehe hizo mshtakiwa alitakatisha kiasi hicho cha fedha huku akijua zimetokana na zao la kusaidia genge la uhalifu na kukwepa kodi.
3
Wanajeshi wa Afrika mashariki wanaingia tena vitani leo baada ya mmoja wao (Uganda) kuanza vyema mashindano hayo, na leo ni zamu ya Kenya na Tanzania kutupa karata zao dhidi ya Senegali na Algeria. Hali katika timu ya Taifa ya Kenya yaani Harambee Stars ni shwari kuelekea mechi hii ya dhidi yaAlgeria , cheki hapa dondoo muhimu kulekea mchezo huo; WACHEZAJI WA KUWAANGALIA Algeria – Riyad Mahrez Anaingia kwnye mashindano hayo tayari akiwa na morale ya hali ya juu kwani ndo wametoka kuchukua ubigwa wa ligi hivi majuzi na club yake ya Manchester City . Mahrez katika michezo nane iliyopita amehusika katika magoli 5 katika AFCON , kafunga matatu na kutenga mengine mawili. Kenya – Michael Olunga Ameifungia club yake ya Kashiwa Resol ya nchini Japan magoli 6 katika michezo 11 ya timu hiyo, Michael anaingia katika michuano hii akiwa vyema kabisa, na anatarajiwa kuiongoza vyema Kenya kama alivyofanya wakati wa mechi za kufuzu. FACTS MUHIMU. 1.Hii itakua mara ya 18 Algeria anashiriki michuano hii ya AFCON. Walishawahi nyakua kombe ili mwaka 1990 kwenye ardhi ya nyumbani kwao baada ya kuandaa. 2.Katika michezo 13 waliyowahi kucheza kwenye mashindano hayo wana clean sheet moja tu, ambao ulikua ni ushindi wa 2-o dhidi ya Senegal mwaka 2015. 3.Kenya wanashiriki kwa mara ya 6 michuano hii , hii ni kwa mara ya kwanza kwanzia 2004 4.Harambee  Stars hawajawahi kuvuka hatua ya makundi, na tangia washiriki walishawahi kushinda mchezo mmoja tu wa goli 3-0 dhidi ya Burkina Faso. 5. Algeria wako nafasi ya 66  na Kenya wako nafasi ya 105 kwenye viwango vya ubora vya Fifa.
4
AVELINE KITOMARY -DAR ES SALAAM NDOTO za mtoto Abdul Mohamed (10) zimefifia baada ya kupata ajali miaka minne iliyopita na kushindwa kuendelea na masomo, huku familia yake na ya dereva wa gari lililomgonga zikivutana. Baba wa mtoto huyo, Mohamed Hamis, anayeishi  Ulongoni B, Kata ya Gongo la Mboto, Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, anadai familia ya aliyemgonga imekataa kumuhudumia mtoto wake na yeye hana uwezo. Kwa upande wa familia ya dereva aliyemgonga mtoto huyo, inadai ilisimamia matibabu hadi kumfikisha Hospitali ya Taifa Muhimbili na afya yake ikaanza kuimarika, lakini baadaye wazazi wake wakamkatisha matibabu na kuanza kumpa tiba za kienyeji. ILIVYOKUWA Imeelezwa kuwa Aprili 3 mwaka 2016 majira ya asubuhi, maeneo ya Ulongoni B, gari lililokuwa likiendeshwa na Kilimo Joseph, lilimgonga mtoto huyo na kumsababishia majeraha mwilini na kushindwa kuendelea na masomo. Mtoto huyo aliliambia gazeti hili kuwa gari hilo lilimgonga wakati akicheza na wenzake. “Sisi tulikuwa tunacheza, akachukua gari akaja akanigonga, wakanipeleka hospitali wakanipima kipimo kimoja wakaniacha, nataka kupata matibabu niendelee na kusoma,” alisema Abdul. Baba mzazi wa mtoto huyo, Hamis, alisema mtoto wake tangu amepata ajali hakupata huduma kwa familia ya mtu aliyemgonga kwa kipindi chote jambo lililomlazimu kwenda hadi mahakamani ili kuweza kupata haki ya kutibiwa. “Tumejitahidi mpaka tulipoishia, tumefuatili hiyo kesi lakini hatujui imeishia wapi, tumekwenda mahakamani tunaambiwa tufuatilie hukumu na uwezo wetu ni mdogo, tunaomba Watanzania wenzetu watusaidie,” alisema Hamis. “Nimekuwa mtu wa kuzungushwa mpaka kesi imeenda mahakamani bila kupewa taarifa, mara ya mwisho kwenda polisi naambiwa kesi ipo mahakamani, nilipofika mahakamani naambiwa nimechelewa kesi imeisha niandike barua ya kumaliza kesi na nipewe karatasi ya hukumu, ndipo nilipomwambia mimi sijui kuandika,” alisema Hamis. Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ulongoni, Petro Masalale, alisema mwanafunzi huyo alimsajili mwaka 2016 na kwa bahati mbaya alipata ajali ambayo ilihatarisha taaluma ya mtoto huyo. Mwalimu Masalale alidai kuwa aliyesababisha ajali hakutoa ushirikiano kwa mtoto huyo. “Aliyesababisha ajali hajatoa ushirikiano, kwani yeye kama mwanadamu alipaswa kutoa mchango wake wa kumsaidia mtoto huyo jambo ambalo hajalitimiza,” alidai. Mjumbe msaidizi wa eneo la Ulongoni B, Mtaa wa Mji Mpya, Samson Makanke, alisema mwenye gari lililomgonga mtoto huyo aliitwa na kusema atamuhudumia, lakini akamtelekeza wakati akiwa Hospitali ya Muhimbili. Baadhi ya wakazi wa eneo hilo walisema wameshangazwa na kitendo cha kinyama anachofanyiwa mtoto huyo kutokana na familia ya aliyemgonga kutomuhudia ili aweze kupona. Hata hivyo, mmoja wa familia ya aliyemgonga mtoto huyo, Halima Athumani, alikanusha tuhuma hizo na kusema walikuwa wakimuhudumia mtoto huyo ila tatizo mzazi wake alikuja kuchanganya matibabu ya hospitalini na imani za kishirikina. “Aliyemgonga huyo mtoto ni mvulana ambaye nilikuwa nakaa naye na mtoto alivyogongwa tulikuwa tunajenga, tukahairisha kwanza ili kumuhudumia. “Tulianza kumuuguza akiwa hospitali ya jeshini baadaye tukaenda Amana hadi Muhimbili tulimuhudumia. “Baada ya hapo mtoto akawa anaendelea vizuri tu na alikuwa anafanya mazoezi Muhimbili, baadaye wakamwachisha mazoezi wakawa wanasema mtoto wao kalogwa, wakaanza kumpa matibabu ya kijadi ndiyo walivyorudi tena Muhimbili wakaambiwa waanze tena mwanzo,” alisema Halima. Alidai baada ya mtoto kuendelea kuzidiwa, walimpeleka polisi ambako waliwaambia wazungumzie jambo hilo nyumbani. “Baada ya kutoka polisi katika mazungumzo mwanzoni tulikubaliana kuwa nitanunua pikipiki ili ifanye biashara mtoto apate matibabu na mahitaji, wakakubali. “Lakini baadaye wakaja kubadilisha maamuzi, wakaniambia niwanunulie kiwanja halafu niwajengee nyumba, mimi nikawaambia uwezo huo sina,” alidai Halima.
3
Katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi jana Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Chamwino, Aithan Chaula alisema ekari 300 nyingine zimeongezwa ambapo wananchi wanaoishi vijiji karibu na shamba hilo wamegawiwa ekari moja kila moja ambapo sasa wameanza kusafisha na kuchimba mitaro.Sasa shamba litakuwa la ekari 600.“Kama tutakwenda sawa sawa mwisho wa mwaka huu shamba lote litakuwa limepandwa,” alisema.Alisema wananchi waliopata maeneo hayo wanachimba mitaro kwa nguvu zao kwani waliona mafanikio waliyopata wenzao 300 wa kwanza wanaolima zabibu katika eneo hilo.Alivitaja vijiji ambavyo wananchi wake wamepatiwa maeneo kwa ajili ya kulima zabibu kuwa ni Chinangali 2, Manchali, Makoja, Buigiri, Mlebe na Chamwino.Alisema wakulima wa kwanza 300 ni wanachana wa Fune Saccos na Chabruma Amcos ambao wamekuwa wakipata mikopo kwenye taasisi za kifedha, hali ambayo iliwavutia wananchi wengi zaidi na kuona faida za kilimo cha zabibu.Alisema shamba hilo lina miundombinu ya umwagiliaji kwa kutumia matone na ni moja ya mashamba makubwa ya zabibu katika mkoa wa Dodoma.Pia alisema kuna shamba jipya la zabibu Mvumi Makulu ambapo kuna ekari 323 na wananchi watachimba mitaro kwa nguvu zao huku wakisaidiwa na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP).Chaula alisema lengo la kuwa na mashamba makubwa kwenye eneo moja kunarahisisha upatikanaji wa huduma za ugani, miundombinu ya maji, umwagiliaji, upatikanaji wa mikopo na kwenda pamoja katika kuongeza thamani ya zao husika.
5
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema suala la kuwaondoa kazini watumishi wa umma ambao ni wazembe, wala rushwa na wasiotimiza majukumu yao ipasavyo ni endelevu.Amesisitiza kuwa serikali inahitaji watumishi wenye heshima na nidhamu ya kazi ili waweze kuwatumikia wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote iwe wa kiuchumi, kidini au kikabila. Waziri Mkuu alisema hayo jana wakati akihutubia wananchi katika Kongamano la Kumpongeza Rais John Magufuli kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/20. Kongamano hilo limeandaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ili kumpongeza Rais John Magufuli lilifanyika katika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.Alisema serikali imejipanga vizuri katika mapambano dhidi ya rushwa. Aliwataka wananchi watoe taarifa, iwapo watabaini uwepo wa watumishi wanaojihusisha na rushwa. “Watumishi wa umma tunataka watambue kwamba wao ni watumishi wa wananchi, hivyo hawana budi kutambua wajibu wao ambao ni kumtumikia mwananchi ipasavyo,” alisema. Alisema kuwa serikali imepiga hatua kubwa katika vita dhidi ya rushwa, ambapo kwa Afrika, Tanzania inaongoza kwa mujibu wa ripoti ya taasisi ya Transparency International.Katibu Mkuu wa UWT, Queen Mlozi alisema kongamano hilo ni muendelezo wa kongamano zingine za kumpongeza Rais, zilizofanyika kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya na Unguja na Pemba. Alisema viongozi hao wameonesha dhamira ya kweli ya kuwaletea wananchi maendeleo. “Tutaendelea kushirikiana na viongozi wetu na hatupo tayari kugawanyika” alisema.Awali, mawaziri na naibu mawaziri mbalimbali, walipata fursa ya kuelezea namna ilani ilivyotekelezwa katika maeneo mbalimbali kupitia wizara zao. Katika kongamano hilo, viongozi na wanachama wa vyama mbalimbali walivihama vyama vyao na kujiunga na CCM akiwemo na aliyekuwa Katibu wa Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.
3
INAWEZEKANA upo katika uhusiano na mpenzi ambaye hukumwelewa vizuri mwanzoni, lakini sasa unagundua kwamba amepoteza uwezo wa kupenda kama ilivyokuwa awali. Ni vigumu sana kugundua hili mapema, lakini ukimchunguza na kuwa mkweli kwake, ni rahisi kukueleza ukweli huu uliojificha moyoni mwake. Pengine wakati unakutana naye, alikukatalia akisema muda wa kuwa na mpenzi bado, lakini ukaendelea kumsumbua na kukukubalia, mwisho wa siku ukagundua hafurahii uhusiano wenu. Hili huwa tatizo kubwa sana kwa walio wengi. Wakati mwingine yawezekana ukawa unafanya bidii ya kumshawishi mpenzi mpya lakini akawa katika tatizo hili. Kila siku anakuzungusha, lakini siku moja akaamua kukueleza ukweli, kwamba anashidwa kukupenda! Hiyo ni hatua nzuri kwako, maana yamkini sasa unaweza kusuka mbinu mpya za kurejesha ule upendo wake wa awali uliotoweka ili muweze kuanzisha uhusiano ulio na nguvu. Katika vipengele vifuatavyo, vitakusaidia kwanza kung’amua mpenzi ambaye amepoteza upendo wake wa awali au patna ambaye una mpango wa kuanzisha uhusiano naye lakini hana uwezo wa kupenda tena kutokana na sababu mbalimbali. Sasa hebu twende  katika vipengele vifuatavyo, bila shaka kuna kitu kipya utakijenga kichwani mwako.   KWANINI HILI HUTOKEA? Ni muhimu kwanza kujua sababu za kupoteza ule uwezo wa kupenda uliokuwa mwanzo. Angalau kwa kujua, itakusaidia kusogea kwenye ukweli na kuifuata hatua nyingine muhimu zaidi. Tatizo la kutokuwa na uwezo wa kupenda, limekuwa likiwasumbua wengi sana siku hizi (hasa wanawake). Sababu kubwa zaidi ni kuwa na uhusiano wenye historia mbaya katika kipindi kilichopita. Mwanamke aliyeachwa na wanaume watatu kwa kipindi cha miezi miwili, hawezi kuwa na uwezo wa kupenda kwa asilimia 100 kama yule ambaye ndiyo kwanza anaanza uhusiano. Mwanamke aliyeachwa na mwanaume wake aliyedumu naye kwa miaka minne, anaweza kuwa bora zaidi katika uhusiano mpya akitaka kuokoa maisha yake ya kimapenzi kuliko yule ambaye ametoswa mara nyingi zaidi. Yapo mengi yanayosababisha hilo, lakini kwa uchache ni pamoja na vifuatavyo;   (i) Anahisi havutii Mara nyingi wasichana wakiachwa, hukuchukulia kwamba huenda hawana mvuto sana. Kwahiyo anahisi hata kama atakupenda, akitokea mwenye mvuto zaidi yake, utamtosa kama alivyofanya aliyepita!   (ii) Ugonjwa wa moyo Inawezekana ameshaumizwa sana huko nyuma na kila anapokuangalia anahisi kuteswa tena na hivyo anaogopa tena kupata ugonjwa wa moyo! Ana mashaka, hana amani na mapenzi tena, sababu kubwa ni historia iliyopita.   (iii) Walewale! Lakini kubwa zaidi ni kwamba, mtu akiwa katika athari hii, akili yake yote inamwambia kwamba wote wanaweza kuwa sawa na waliopita. …uking’atwa na nyoka, hata unyasi ukikugusa unashtuka rafiki zangu! Hisia hizo zinaweza kumfanya akaogopa kuwekeza moyo wake tena kwako.   UTAMTAMBUAJE BASI? Ni afadhali uwe katika hatua za kumfuatilia, kabla hujajua chochote ukagundua wazi kwamba huyu ana tatizo la kupenda, lakini ukishaingia katika uhusiano naye, ni vigumu sana kujua, maana unaweza kuhisi anakudharau kumbe mwenzio ni mgonjwa! Lakini hapa, zipo njia za kitaalam kabisa ambazo zinaweza kukufanya ugundue mpenzi wako ana tatizo la ugonjwa wa kupenda! Hebu tuone…   (i) Siyo muwazi Sifa ya kwanza kabisa ni kwamba, hataki kukupa nafasi ya kumjua vizuri, anakuogopa, maana ukijua udhaifu wake unaweza kumtenda na kumfanya aishi mpweke kwa mara nyingine. Ni msiri sana, hataki ujue ratiba zake na mambo yake mengi anafanya kwa kushtukiza.   (ii) Anachelewa kupokea simu Hayupo katika penzi la msisimko, kwahiyo hata akiona simu yako anashtuka na kuogopa kupokea haraka. Hana amani ya moyo. Hapendi kukusikia ukisema; “I love you baby!” maana anahisi kama unamuumiza tu. Vinginevyo basi anakuona kama unamzingua tu.   (iii) Mgumu kukuambia anakupenda Ukiwa naye katika mahaba au mtoko, ukimwambia: “Nakupenda sana mpenzi wangu,” yeye anaona shida sana kukujibu anakupenda pia. Sababu kubwa hapa ni majeraha ya moyo. Huwa anahisi kama atakuwa anakudanganya, maana moyo wake una bandeji kila kona. Upo na mgonjwa! Jiandae kupata kitabu changu kipya cha SIRI ZA NDOA YENYE FURAHA kitakachokuwa mitaani hivi karibuni.   Wiki ijayo tutaendelea na mada hii, USIKOSE!
1
MAJERUHI 13 walionusurika katika ajali ya lori lililolipuka na kuua watu 76 hadi sasa hawajitambui, hatua ambayo imefanya ofi si ya Mkemia Mkuu wa Serikali, kuingilia kati ili kumaliza utata ulioibuka kutoka kwa baadhi ya ndugu wa majeruhi hao.Ajali hiyo ilitokea Agosti 10, mwaka huu saa mbili na dakika 20 asubuhi baada ya lori aina ya Scania lenye namba za usajili T 717 DDF, likiwa na trela namba T 645 CAN, likiwa limebeba mafuta ya petroli na dizeli kupinduka.Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Aminiel Aligaesha alisema kuna baadhi ya watu wamejitokeza, ambao si ndugu wa marehemu wala majeruhi na kuzua utata.“Tumealika watu waje kutambua miili au majeruhi ambao hawajitambui, cha kushangaza kuna watu ambao hawana uhusiano na ndugu lakini wamekuja sasa unakuta mtu mmoja wanajitokeza watu watatu mpaka watano na hawajuani,” alisema.Aligaesha alisema kuwa kufuatia hali hiyo, wameomba msaada kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ili waweze kuchukua vinasaba kwa ndugu waliojitokeza pamoja na majeruhi, ambao hawajitambui, pamoja na maiti.“Mpaka sasa wagonjwa wote 13 ambao hawajitambui wameshachukuliwa vinasaba vyao, na ndugu zaidi ya 45 wameshachukuliwa vinasaba ambao tutalinganisha na miili ambayo ipo mochwari na wale ambao hawajitambui,” alisema.Meneja wa Maabara ya Vinasaba (DNA) kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Hadija Mwema alisema sampuli linganishi zimechukuliwa kutoka kwa wazazi baba, mama na kuna baadhi ambao wazazi wao walishatangulia mbele za haki, hivyo wanachukua vinasaba kwa watoto na ndugu wa karibu kama baba mdogo, baba mkubwa, kaka ama dada.“Kuna baadhi ya wenzetu wazazi wameshatangulia mbele za haki na kuna wengine bado hawajawa na watoto, teknolojia ya vinasaba inawezesha utambuzi kwa wale ndugu wa karibu kabisa, ndio zoezi linaloendelea hapa sasa,”alisema.Alisema sampuli ya vinasaba imeshachukuliwa kwa miili yote, na pia ambao hawajitambui pia sampuli zimechukuliwa, kwa lengo la kulinganisha. Wakati huo huo, Eligaesha alisema majeruhi mwingine amefariki dunia usiku wa kuamikia jana na hivyo kufanya idadi ya waliopoteza maisha kufikia 76.Alisema majeruhi 13 walionusurika hali zao ni mbaya na wamelazwa katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) wakiwa hawajitambui, huku 25 wakiwa wanaendelea vizuri. Alisema waliofariki dunia katika Hospitali ya Muhimbili hadi sasa ni wanane.“Hadi leo Agosti 13, hiyo ndiyo idadi ya wagonjwa waliolazwa MNH, na wale ambao wamefariki dunia tayari miili yao imepelekwa Morogoro na mmoja umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hapa Muhimbili,” alisema Aligaesha.Wagonjwa waliofikishwa hospitalini hapo baada ya ajali walikuwa 45, wanaume wakiwa 41 na wanawake wanne. Tume ya uchunguzi yaanza kazi Katika tukio lingine; Waziri wa Nchi , Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama amesema tayari Waziri Mkuu amekamilisha kazi yake ya kuunda tume ndogo ya wataalamu, ambayo imeanza kazi zake na amewahakikishia Watanzania kuwa baada ya kukamilisha shughuli zake taarifa rasmi itatolewa kwa wananchi.Waziri Jenista alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari nje ya viwanja vya jengo la kuhifadhia maiti la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, ambapo pia timu ya Kitaifa ya Maafa ilikabidhi rasmi timu ya maafa ya Mkoa wa Morogoro kuendelea kufanya kazi na hiyo wakati ya kitaifa ikiendelea kusimamia na kufuatilia wa maafa hayo.Jenista alilazimika kutoa ufafanuzi wa shughuli za tume ndogo ya wataalamu, iliyoundwa na Majaliwa ambayo aliipa siku sita kuchunguza namna ya uwajibikaji wa viongozi uliochukuliwa kabla ya ajali ya lori mafuta na kusababisha vifo vya watu wengi na kujeruhi wengine. Waziri Mkuu alitoa agizo hilo Agosti 11 mwaka huu, alipotoa salamu za pole kwa niaba ya Rais John Magufuli.Alisema ripoti ya tume hiyo, itaisaidia serikali kuchukua hatua ya viongozi na watendaji walishindwa kuwajibika kikamilifu kutokana na ajali hiyo. Jenista alisema: “Tutatoa taarifa rasmi kwa sababu tayari Waziri Mkuu amekamilisha na amekabidhi jukumu kwa tume na tutaweka utaratibu wa kuripoti kazi za tume”.
3
SEOUL, KOREA KUSINI JARIBIO jipya la Korea Kaskazini kurusha kombora limeshindikana baada ya kuripuka muda mfupi tu lilipofyatuliwa jana, ikiwa ni  siku moja tangu ilipoonesha hazina yake ya makombora katika gwaride kubwa la kijeshi. Kushindwa  huko , ambako  kunaonekana  kwa  umma  kama  kitu cha  fadhaa  kwa  serikali  ya  nchi  hiyo, kumekuja  huku  hali  ya wasi  wasi  ikiongezeka   katika  rasi ya Korea kuhusu  dhamira ya  taifa hilo kujipatia  silaha  za  nyuklia. Hata  hivyo  haikuwezekana  kufahamika mara  moja  aina gani  ya  kombora hilo. Jaribio  hilo  limekuja baada  ya  Korea  Kaskazini  kuonesha karibu  makombora 60  ikiwamo jipya lenye uwezo wa kuvuka  mabara wakati wa  gwaride siku  ya  Jumamosi  kuadhimisha  miaka  105 ya  kuzaliwa  kwa mwasisi  wa  taifa  hilo,  Kim II-Sung. Sherehe  hizo zilifanyika  mbele ya kamera za mashirika  ya habari duniani  yaliyoalikwa na ambayo  yalikuwapo pia wakati wa jaribio  la  kurusha  kombora  hilo  lililoshindwa. Aidha kushindwa  kwa kombora  hilo  kunakuja  saa chache  kabla  ya ziara  ya  Makamu  wa  Rais  wa  Marekani,  Mike  Pence  nchini hapa,  ambako  suala la Korea Kaskazini  litakuwa  ajenda  ya  juu. Korea  Kaskazini  ina  tabia  ya  kurusha  makombora  kuadhimisha sherehe  muhimu  za  kisiasa, ama  kama  ishara  ya  ukaidi  wakati  maafisa  wa  ngazi  ya  juu  wa  Marekani  wanapofanya ziara  eneo  hilo.
2
MAOFISA wa Afya nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC) wamethibitisha kuwa mtoto wa kike mwenye umri wa siku sita, aliyethibitika kupata maambukizi ya ugonjwa wa ebola, amepona ugonjwa huo.Mama yake na mtoto huyo, Benedicte ambaye madaktari wamembatiza ‘mtoto wa miujiza’ alikuwa ameambukizwa ugonjwa wa ebola na alifariki wakati anajifungua. Benedicte alianza kuonesha dalili siku chache baada ya kuzaliwa na madaktari walikuwa na wiki tano tu kumtibia na kuhakikisha anakuwa hai.Baba na shangazi yake walimpeleka nyumbani siku ya Jumatano wiki iliyopita. Ebola ni ugonjwa hatari unaosababisha kifo kwa haraka na huambatana na homa kali, kutapika, kuharisha, na kutoka damu nje na ndani.Nusu ya wanaoambukizwa hufariki, lakini watoto ni ngumu sana kupona. Tangu ugonjwa huo ulipolipuka tena nchini DRC, sasa hivi kuna taarifa za kesi 27 za ugonjwa huo kwa watoto ambao walikuwa hawajafikisha mwaka mmoja na 21 walifariki. Taarifa kama za kupona kwa Benedicte ni adimu sana. Benedicte alizaliwa Oktoba 31, mwaka huu, na alikuwa akitibiwa katika kituo cha ebola huko Beni, mji ulioathirika sana na mlipuko wa ugonjwa huo DRC. Mtoto huyo, ndiye mgonjwa mdogo zaidi ambaye madaktari na watu wanaojitolea wamemhudumia.Mtoto huyo wa kike sasa anajulikana kama ‘muujiza wa Beni’. Ebola ni ugonjwa unaosambaa haraka na husababisha vifo vya asilimia 50 ya waathirika. Dalili za awali ni homa ya ghafla, uchovu kupita kiasi, maumivu ya mishipa na koo. Dalili za hatari ni kutapika, kuharisha, na kwa kesi zingine ni kutoka damu ndani na nje ya mwili. Ugonjwa huo, huwapata binadamu wanapogusana na wanyama walioathirika wakiwemo sokwe mtu, popo na paa.
3
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imesitisha mpango wa kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma stashahada (Diploma) kuanzia mwaka wa masomo 2018/19. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru, ilisema mpango huo umesitishwa kama ilivyotangazwa na Serikali. Mei 10, mwaka huu, HESLB ilitoa mwongozo unaosimamia utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/19. Pamoja na mambo mengine mwongozo huo unaeleza bodi hiyo itaanza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa stashahada na kuwa utaratibu wa kuomba mikopo kwa wanafunzi hao ungetolewa baadae. Taarifa hiyo, ilisema hatua hiyo imechukuliwa ili kuhakikisha Sh bilioni 427.5, zilizotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka 2018/19, zinaelekezwa kwa wanafunzi wenye mikopo hivi sasa na waombaji wapya wenye sifa za kujiunga na kozi za shahada tu ambao ndiyo walengwa wakuu. “Tunatoa wito kwa wanafuzi wote wenye sifa za kujiunga na masomo ya shahada katika taasisi za elimu ya juu na  wahitaji wa mikopo kuhakikisha wanasoma kwa makini mwongozo wa utoaji mikopo na kuuzingatia,”ilisema taarifa hiyo. Takwimu za mwaka 2017/18, zinaonyesha karibu maombi 10,027 ya mikopo yaliyowasilishwa ndani ya bodi yalikuwa na upungufu kama vile kutosainiwa na kukosa viambatanisho sahihi.
0
Akikabidhi vifaa hivyo Meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel, Hawa Bayumi alisema, vifaa hivyo vitamuwezesha Godfrey kukuza biashara na kuongeza kipato cha biashara yake.Bayumi alisema mpango huo wa kuwawezesha wajasiriamali vifaa ni sehemu ya mpango wa kampuni hiyo wa kuwawezesha vijana ambao wengi ni wateja wao.“Sisi kama kampuni ya mawasiliano tumeona ni vizuri kushirikiana na wajasiriamali na hasa vijana wenye umri kati ya miaka 18-24 ili kuhakikisha tunawawezesha na kukuza mitaji yao ya biashara kwa mafunzo na vifaa,” alisema Meneja huyo.Awali akipokea msaada huo Manjavila aliishukuru Airtel kwa vifaa hivyo na kuahidi kuendeleza zaidi biashara hiyo ili kutimiza ndoto zake za kuwa mfanyabiashara mkubwa.“Sikuamini kama naweza kufikia malengo yangu katika biashara hii, naahidi kuongeza juhudi na kutumia vyema msaada huu ili kuhakikisha nakuza na kuendeleza biashara yangu,” alisema Manjavila.Mama mzazi wa Manjavila, Aziza Nachenda, alisema amefurahishwa na msaada alioupata kijana wake.“Hatuamini kama leo ndugu yetu ameweza kuwa miongoni mwa wajasiriamali wakubwa kwani imekuwa ni ndoto yake ya muda mrefu na sisi tunadhani sasa atafikia malengo yake,” alieleza ndugu wa mshindi huyo.Kampuni ya simu ya Airtel inazunguka nchi nzima kukutana na vijana kwa lengo la kuwapa elimu ya ujasiriamali na kisha kutoa uwezeshaji kwa vijana.
5
Halmashauri ya Wilaya ya Urambo mkoani Tabora inahitaji mwekezaji wa kuiendesha hoteli iitwayo Urambo Motel ili kuongeza mapato.Jengo la hoteli hiyo mjini Urambo lenye vyumba 24 kwa sasa halitumiki.“Tumekosa mwekezaji, limechakaa na linahitaji nguvu kubwa sana ya kuweza kuwekeza pale. Kwa hiyo tukipata mwekezaji pale akaweka labda hoteli kubwa inaweza ikawa inakusanya viongozi mbalimbali au wawekezaji wageni mbalimbali itaweza kumfanya yule mwekezaji apate kipato kikubwa na inaweza ikasaidia sana kuweza kuitangaza wilaya yetu ya Urambo nawageni wageni wakapata mahala pazuri pa uhakika pa kufikia” amesema Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Adam Malunkwi.Amesema ofisini kwake mjini Urambo kuwa, Halmashauri hiyo pia inahitaji mwekezaji wa kujenga stendi kubwa ya kisasa. Kwa mujibu Malunkwi, wameshaandaa michoro kwa ajili ujenzi huo unaohitaji uwekezaji mkubwa.Amesema, Urambo pia inahitaji mwekezaji ajenge kiwanda cha ngozi ili kuongeza thamani ya ngozi kwa kuzalisha bidhaa zinazotokana na ngozi.Malunkwi amesema, kuna ng’ombe zaidi ya 121,000 wilayani humo hivyo wanahitaji pia mwekezaji ajenge kiwanda cha kuzalisha bidhaa zinazotokana na mazao ya mifugo yakiwemo maziwa.Amesema, kila siku ng’ombe sita hadi 10 wanachinjwa mjini Urambo hivyo kuna ngozi za kutosha kwa kuwa vijijini nako wanyama hao wanachinjwa.
5
TIMU ya taifa ya soka ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens imepania kuendeleza rekodi ya kufi ka fainali iwapo tu kama itafanya vizuri katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya Uganda leo.Timu nne zilifanikiwa kutinga hatua hiyo michuano ya Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda na Burundi. Nusu fainali ya kwanza itachezwa leo kuanzia saa 7 mchana kwenye Uwanja wa Azam Complex kati ya Kenya na Burundi kisha nusu fainali ya pili Kilimanjaro Queens itachuana dhidi ya Uganda saa 10:00 jioni.Akizungumzia maandalizi ya kikosi chake Kocha Mkuu wa Kilimanjaro Bakari Shime alisema wako tayari kuwakabili wapinzani wao Uganda na wameandaa mbinu nyingine mpya za kuwabana ili kupata matokeo mazuri.“Tutakuja na staili nyingine, vijana wote wako salama, hata wale wote waliokuwa na shida na wasiokuwepo wamerejea, kikosi kimetimia kwa asilimia 100,”alisema.Alisema wameona ubora na madhaifu ya timu pinzani lakini pia, amerekebisha mapungufu yaliyoonekana katika kikosi chake hivyo, wataingia wakiwa na nguvu mpya. Kwa upande wake Kocha wa timu ya wanawake ya Kenya Jackline Juma alisema wanawaheshimu Burundi ni timu nzuri ila anaamini matokeo yanapatikana ndani ya dakika 90.Awali, Kilimanjaro walifikia hatua hiyo baada ya kuwachapa Sudan Kusini mabao 9-0, Burundi mabao 4-0 na Zanzibar 7-0, huku Uganda ikimfunga Ethiopia 2-1, Djibout 13-0 na kupoteza mbele ya Kenya mabao 3-0. Kwa upande wa Kenya iliifunga Djibouti 12-0, Uganda 3-0 na Ethiopia 2-0 na Burundi iliwachapa Sudan Kusini mabao 5-0, Zanzibar 5-0 na kupoteza kwa Tanzania mabao 4-0.Kufuatia timu hiyo kufanya vizuri, baadhi ya wadau wa Kampuni ya taulo za kike ya Rani ilijitokeza jana na kutoa taulo, sabuni na mafuta kwa timu ya Kilimanjaro kutokana na kuonyesha juhudi.Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Oscar Mirambo alitaja kiingilio cha michezo hiyo kuwa ni sh. 1000 na kuhimiza mashabiki kujitokeza kwa wingi kuunga mkono.Mjumbe wa Cecafa Habimana Aimable alipongeza Watanzania kwa kujitokeza kwa wingi uwanjani, wadhamini na TFF kwa kaundaa mashindano mazuri huku akisema mwaka huu yamekuwa yenye ushindani mkubwa kuliko huko nyuma.
4
Wiki hii tutazungumzia uwajibikaji kwa umma, ambapo serikali kupitia kanuni hizo za utumishi wa umma, zinamuelekeza kila mtumishi wa umma nchini kuwajibika kwa umma wa Watanzania kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.Kama namna mojawapo ya kuwajibika kwa umma ipasavyo, mtumishi wa umma anapaswa kuwahudumia kwa heshima wateja wake wote, ikiwa ni pamoja na watumishi wenzake ambao kimsingi ni wateja wake wa ndani na wale wanaotoka nje ya taasisi kuja kutafuta huduma ambao ndiyo wateja wa nje.Kwa mfano, namna nzuri ya kumhudumia mteja kwa heshima ni kumpokea, kumsikiliza, kumuelimisha pale anapotakiwa kuelimishwa na hatimaye kumpa huduma stahiki kwa ukarimu na upole. Inawezekana kuna wanaofikiri mteja wa nje anapaswa kuhudumiwa kwa heshima zaidi ya yule wa ndani. Kusema kweli, mteja wa ndani pia anahitaji kuheshimiwa kama anavyoheshimiwa yule wa nje.Hapa kuna hatari ya mambo kama utani au kuamini mteja wa ndani yupo tu kwa muda mrefu na hivyo kuna hatari ya kutotoa muda wa kutosha kwa mteja wa ndani. Vilevile, ili kuhakikisha kuwa watumishi wa umma wanawajibika ipasavyo kwa umma, serikali kupitia kanuni za maadili ya umma imewaelekeza watumishi wa umma, kuwahudumia kwa makini zaidi wananchi walioko katika mazingira magumu.Kwa mfano, huduma inatakiwa kutolewa kwanza kwa wateja waliotangulia kufika kwenye eneo la huduma ambapo foleni inaweza kutumika kuwabainisha waliowahi. Hata hivyo, watumishi makini wanatakiwa kuwabaini na kuwapa kipaumbele watu kama wazee, wajawazito, watoto, wagonjwa, na watu wenye ulemavu. Hili siyo jambo gumu kwavile mara nyingi watu wanaopanga foleni, wanakuwa na utulivu wa hali ya juu, pale wanapoona na kuridhika kuwa kwa kweli aliyerushwa katika foleni ana hali inayohitaji kusaidiwa.Vilevile, serikali kupitia kanuni za maadili ya utumishi wa umma, inawataka watumishi wa umma kutoa ufafanuzi au maelekezo kuhusu sheria, kanuni na taratibu zinazowaongoza katika utekelezaji wa majukumu yao, ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma mbalimbali pale wananchi wanapoomba kufahamishwa. Kwa mfano, mwananchi anapotaka kupata leseni ya kuendesha gari, watumishi wa umma wanaohusika na utoaji wa leseni hizo wanaweza kuwa chanzo muhimu cha mteja kujifunza mambo ya sheria, kanuni na taratibu zinazotakiwa kufuatwa ili kumwezesha mteja huyo kupata leseni anayotaka. Kwa kufanya hivyo, upo uwezekano wa baadhi ya watumishi kuona kama wanapoteza muda wa kazi.Hata hivyo, ni wazi kuwa mtu anayeelimishwa juu ya mambo ya msingi na akaelewa, hata kumhudumia inakuwa ni rahisi zaidi. Jambo kubwa na la muhimu pia katika kuwajibika ipasavyo kwa umma, ni kwa watumishi wenyewe kutambua bayana kwamba wanapaswa kutekeleza wajibu wao wakijihesabu kwamba wao ni watumishi wa umma. Sasa kwa vile umma maana yake ni wananchi wote, hii inawasaidia watumishi kutambua kwamba wameajiriwa kutekeleza majukumu mbalimbali yanayolenga kuwatumikia wananchi wa Tanzania kwa namna mbalimbali zilizowekwa kisheria.Katika moja ya makala zilizopita, nilipata kusema kuwa mara nyingi mtumishi wa umma anaweza kujikuta akiwa na shinikizo la kijamii la kutoa huduma kwa kupendelea watu wenye nafasi kubwa kifedha, kimadaraka na hata wale wenye uhusiano naye wa damu na urafiki. Katika makala hayo nilisema kuwa suluhisho pekee ni kwa mtumishi husika kutoa huduma iliyotukuka kwa wote ili kila mmoja kwa namna yake atoke ameridhika.Kwa mantiki hiyo hiyo, mtumishi wa umma anapaswa kutoa huduma kwa heshima kubwa kwa wale wenye nafasi za juu na wale wenye nafasi za chini. Tafiti mbalimbali zimethibitisha kuwa, watu wenye mafanikio makubwa duniani ni watu ambao wamekuwa wakiheshimu walioko juu yao na wale walioko chini yao kwa maana ya kuishi nao vizuri. Hii inaelezea ni kwanini watu waliofanikiwa kufikia nafasi za juu kama vile nafasi za kisiasa, kiserikali, kibiashara na nyinginezo, kwa kiasi kikubwa wanakuwa ni watu wenye kuheshimu walioko chini yao.
3
PARIS, UFARANSA BEKI mpya wa klabu ya PSG, Dani Alves, ameingia kwenye historia ya wachezaji waliotwaa mataji mengi duniani baada ya juzi kuongeza taji la 34 akiwa na klabu hiyo mpya. PSG juzi ilishuka dimbani dhidi ya wapinzani wao Monaco na kufanikiwa kushinda mabao 2-1 katika mchezo wa kuwania taji la French Super Cup, beki huyo alifunga bao moja katika ushindi huo. Alves amejiunga na klabu hiyo katika kipindi hiki cha majira ya joto akitokea klabu ya Juventus ya Italia na huku aliitumikia klabu hiyo msimu mmoja na kutwaa jumla ya mataji matatu ikiwa pamoja na lile la Ligi Kuu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34, alikuwa anahusishwa kutaka kujiunga na klabu ya Manchester City kwa mkataba wa miaka miwili na ilidaiwa kwamba tayari alikuwa amemalizana na kocha wa timu hiyo Pep Guardiola, lakini alishangaza mashabiki baada ya kuonekana mjini Paris akiwa ndani ya klabu ya PSG. Hata hivyo, baada ya kujiunga na klabu hiyo ya PSG, Alves aliomba radhi kwa Pep Guardiola na mashabiki wa Manchester City kutokana na usumbufu aliowapa na alisema kuwa amefanya maamuzi hayo ya kujiunga na PSG kwa ajili ya kwenda kutwaa mataji. Tayari amefanikiwa kuanza na taji ikiwa ni mchezo wake wa kwanza wa kuwania taji tangu ajiunge mapema mwezi huu, taji hilo la French Super Cup linamfanya awe kwenye orodha ya wachezaji watatu duniani ambao wamechukua mataji mengi. Alves anashika nafasi ya tatu, huku nafasi ya kwanza ikichukuliwa na nyota wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazil, klabu ya Barcelona na PSG, Maxwell Andrade mwenye mataji 36, akifuatiwa na Ryan Giggs mwenye mataji 35. Alves mwenye mataji 34 kuna uwezekano wa kuongeza mataji zaidi ya hapo kutokana na uwezo alionao na klabu anayoitumikia, hivyo endapo msimu mpya wa ligi PSG ikifanikiwa kutwaa mataji zaidi ya mawili beki huyo ataweka historia ya aina yake. Nafasi ya nne inachukuliwa na mshambuliaji wa klabu ya Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, akiwa na mataji 33.
4
KHARTOUM – Sudan  WAKATI taarifa mpya zikieleza kuwa watu takribani 30 waliuawa juzi baada ya Jeshi nchini Sudan kushambulia waandamanaji,  viongozi wa kijeshi wamesema wanaondoa makubaliano yaliyokuwepo awali na kuruhusu uchaguzi ufanyike ndani ya miezi tisa. Taarifa hiyo imekuja  wakati jeshi likijikuta likikemewa vikali na mataifa mbalimbali duniani kutokana na uamuzi wake wa kushambulia waandamanaji katika mji wa  Khartoum, ambako imeripotiwa watu takribani 30 wameuawa akiwemo mtoto wa miaka minane huku idadi ya waliopoteza maisha ikitarajiwa kuongezeka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres ametaka uchunguzi ufanyike akisema ameshtushwa na ripoti kuwa maafisa walifyatua risasi hospitalini. Mashambulizi hayo ya sasa yameibuka baada ya Jeshi ya kuwapo kwa makubaliano ya miaka ya mitatu ya kipindi cha mpito ndipo uchaguzi ufanyike. Kiongozi wa Baraza la Mpito la Kijeshi (TMC) ambalo limekuwa likiongoza nchi tangu Rais Omar Al Bashir aondolewa kwa mapinduzi madarakani Aprili mwaka huu, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, alisema katika taarifa yake iliyorushwa kupitia televisheni ya Taifa kuwa wamekubaliana “kusitisha mazugumzo na Alliance for Freedom and Change na kuondoa yote waliyokubaliana”. Aliongeza kuwa uchaguzi utafanyika ndani ya miezi tisa na utakuwa chini ya waangalizi wa kikanda na kimataifa. Akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza la BBC, mchambuzi na Balozi wa zamani wa Uingereza nchini Sudan, Rosalind Marsden alisema uchaguzi huo wa ghafla unaweza kutengeneza njia ya kuurudisha uongozi wa zamani madarakani. ” Hakika pia kuna hatari ya vurugu kuendelea,”  alisema. Baada ya jeshi kuua raia, viongozi walioongoza vuguvugu la kutaka utawala wa kiraia kuongoza nchi hiyo, wamesema wamesitisha mawasiliano na serikali ya mpito ya kijeshi (TMC) na kufanya mgomo. Vikosi vya usalama vilifika maeneo ambayo watu walikua wakiandamana, mapema Jumatatu na sauti za risasi zilisikika kwenye picha za video. Katika taarifa yake iliyosomwa kwa njia ya televisheni ya taifa, Jeshi limeeleza masikitiko yake kwa namna hali inavyozidi kuwa mbaya na kusema kuwa operesheni ilikua imewalenga wanaotia dosari hali ya usalama wa nchi. Jeshi limesema limekuwepo kwa ajili ya kulinda raia. Awali, wanaharakati wamesema vikosi vya usalama waliizunguka hospitali moja mjini Khartoum na kufyatulia risasi hospitali nyingine. Kamati Kuu ya madaktari wa Sudan, walio karibu na waandamanaji wamesema mbali a watu 30 waliouawa akiwemo mtoto wa miaka minane mamia ya watu wamejeruhiwa huku idadi ikitarajiwa kuongezeka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amezitaka mamlaka za Sudan kufanya uchunguzi na kuchukua hatua dhidi ya wale waliohusika. Pia amelaani matumizi ya nguvu kuwatawanya waandamanaji, na kushtushwa na ripoti kuwa vikosi vya usalama kufyatua risasi kwenye hospitali. Shirika la habari la Sudan limesema mwendesha mashtaka ameunda kamatai kufanyia uchunguzi matukio hayo. Waandamanaji wamekua wakipiga kambi nje ya jengo la makao makuu ya jeshi tangu Aprili 6  mwaka huu, siku tano kabla ya kuangushwa kwa utawala wa Bashir. Kabla ya uamuzi wa sasa wa uchaguzi mwezi uliopita, waandaaji na majenerali watawala walikubaliana kuhusu muundo wa serikali mpya na muda wa mpito wa miaka mitatu kuelekea kwenye utawala wa kiraia.  
2
 FRANKFURT, UJERUMANI TAKRIBAN watu 40 wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya corona baada ya kuhudhuria ibada kanisani katika mji wa Frankfurt. Idara ya afya katika mji huo imesema mtu mmoja kati ya hao 40 ndiye yuko hospitalini ilhali wengine sio wagonjwa. Wakati huo huo mamlaka katika mji jirani wa Hanau ulio Mashariki mwa Jiji la Frankfurt imesema watu wapatao 16 kutoka mji huo wameambukizwa na virusi vya corona baada ya kuhudhuria ibada ya kanisani mjini Frankfurt. Ili kuzuia maambukizi zaidi, mamlaka ya mji huo wa Hanau imefutilia mbali hafla nyengine iliyokuwa imepangwa kufanyika jana Jumapili katika mji huo. WALIOAMBUKIZWA AFRIKA WAPINDUKIA 100,000  Wakati huo huo, takwimu za hivi karibuni za Kituo cha Kinga na Udhibiti wa Magonjwa cha Afrika (Africa CDC) zinaonyesha kuwa, idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona barani Afrika imezidi 100,000. Kwa mujibu wa taarifa ya Africa CDC hadi kufikia Jumamosi Mei 23, kesi zilizothibitishwa rasmi za corona au Covid-19 barani Afrika ni 103,933. Aidha jumla ya waliofariki kutokana na Covid-19 barani Afrika ni 3,183 huku waliopona baada ya kupata matibabu wakiwa ni 41,576. Kituo cha Africa CDC kimeongeza kuwa hadi sasa virusi vya corona vimesambaa kwenye nchi zote za Afrika, na eneo la Kaskazini mwa Afrika limeathirika zaidi. Mkurugenzi wa WHO barani Afrika Daktari Matshidiso Moeti alisema kwa sasa janga la Covid-19 halijaibua maafa makubwa Afrika kwani idadi ya waliofariki ni ndogo ikilikanishwa na maeneo mengine duniani.  Hata hivyo WHO inasema idadi ya waliopimwa Covid-19 barani Afrika ni ndogo kwani hadi sasa kumekuwa na vipimo milioni 1.5 tu na kwa msingi huo nchi nyingi zinahitaji msaada kuongeza idadi ya vipimo.  Afrika Kusini yenye kesi 18,000 za Covid-19 ndiyo nchi yenye idadi kubwa zaidi ya maambukizi barani Afrika. WATOTO MILIONI 80 WAKOSA CHANJO Katika hatua nyingine Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa janga la corona limevuruga mpango wa utoaji wa chanjo za magonjwa ya kupooza (polio), surua na kipindupindu kwa makumi ya mamilioni ya watoto duniani. Katika ripoti yake mpya ya mwishoni mwa wiki, WHO ilisema watoto karibu milioni 80 wenye chini ya umri wa mwaka mmoja wapo katika hatari ya kupoteza maisha iwapo watakosa chanjo hizo. Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema katika taarifa kuwa, “kukatizwa utoaji wa chanjo kutokana na janga la Covid-19 kunahatarisha kusambaratisha mafanikio yaliyopatikana ndani ya miongo kadhaa iliyopita, katika kukabiliana na magonjwa yanayoweza kuzuilika kwa chanjo kama vile surua.”  Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umesema kusimamishwa safari za ndege na kuwekwa sheria kali za kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 (Corona) kumepelekea kusimama kwa sughuli za ufikishaji na utoaji wa chanjo katika nchi zinazohitaji hususan za Kiafrika. Inaarifiwa kuwa, kampeni 46 za utoaji wa chanjo ya kupooza kwa watoto zimesimamishwa katika nchi 38 duniani hususan za Afrika, baada ya nchi hizo kusimamisha safari zake za ndege ili kuzuia ueneaji wa corona. WHO Mei mwaka jana lilitangaza huko nyuma kuwa, huenda likatangaza karibuni hivi kuwa bara Afrika halina tena ugonjwa wa kupooza wa Polio. Awali bara hilo lilikuwa limeanzia kuutokomeza ugonjwa huo kufikia mwaka 2000.
2
Na Festo Polea MWANAMUZIKI Christian Bella ‘King of melody’, amesema kwamba msanii wa bongo fleva, Ablenego Damian ‘Belle 9’, amekosa nyota ya kung’aa ingawa ana uwezo mkubwa wa kuimba kwa kutumia sauti yake. Christian Bella alisema hayo katika kipindi cha ‘Mboni Show’. Alisema kati ya wasanii watatu wanaomvutia kwa kujua kuzitumia sauti zao, Belle 9 ni mmoja wao. Aliwataja wasanii wengine kuwa ni Ali Kiba na Diamond. “Nisiwe mnafiki, Diamond hana sauti nzuri kama Ali Kiba katika kuimba na Ali Kiba nimeshawahi kufanya naye kazi kwa kuimba ‘Live’ sauti yake ni ile ile, ni msanii mwenye uwezo mkubwa wa kuimba ‘live’, lakini Diamond ni mjanja wa kuichezea sauti yake na anafanikiwa kutangaza nchi kimataifa, lazima apongezwe kwa hili,’’ alifafanua Bella. Bella aliongeza kwa kumtaka Ali Kiba kutojisahau muda mrefu, huku akimshauri kutoa nyimbo bila kuhofia lolote, kwa kuwa uwezo wake ni mkubwa na mashabiki wanataka awe anatoa nyimbo mapema. “Lakini licha ya wawili hawa kufanya vizuri, bado sielewi kwa rafiki yangu Belle 9 ana nyimbo kali na sauti yake inakubalika sana, lakini sijui tatizo ni nyota au vipi, napenda sana kazi zake, ni staa kwangu,’’ alijieleza Bella.
1
SERIKALI hupoteza Sh bilioni 31.8 kila mwaka kutokana na uvuvi haramu katika bwawa la Nyumba ya Mungu, linalozungukwa na Halmashauri za Simanjiro mkoa wa Manyara, Moshi na Mwanga mkoani Kilimanjaro.Bwawa hilo lenye ukubwa wa kilometa za mraba 140 lina uwezo wa kuzalisha tani 5,173 za samaki kwa mwaka zenye thamani ya Sh bilioni 36 ikiwa uvuvi endelevu utazingatiwa.Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira alisema jana uzalishaji sasa ni tani za samaki zisizozidi 600 kwa mwaka sawa na asilimia 11 ya uwezo wa bwawa kuzalisha kitoweo hicho.‘’Uzalishaji huu wa tani 600 sawa na asilimia 11, una thamani ya Sh bilioni 4.2, mtaona kiwango hiki ni kidogo na kinatokana na madhara ya uvuvi haramu.... mikoa hii miwili imeendeleza kampeni za kudhibiti uvuvi huo,’’ alisema. Alisema mikoa hiyo imefanya vikao vya ujirani mwema baina ya wilaya zinazozunguka bwawa. Waliazimia kufungwa kwa bwawa kwa miezi sita, azimio ambalo tayari limeshatekelezwa.‘’Kipindi bwawa limefungwa tumefanya doria 85 zilizohusisha maeneo ya majini na nchi kavu kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi ambapo kiasi cha Sh milioni 35.5 zimekusanywa kutokana na zoezi la kudhibiti uvuvi huo haramu, ‘’ alisema. Wachuuzi wa samaki katika soko maarufu la Manyema manispaa ya Moshi, Jabir Abubakar na Musa Swalehe waliomba serikali kudhibiti uvuvi huo badala ya kuwapora samaki sokoni.
3
ALLY BADI- LINDI BAADHI ya wanaume wa Kata  ya  Kilolambwani wilayani  Lindi wamelalamika kuteswa na wake zao kwa kuwashurutisha kufanya kazi kinyume na imani za dini. Wakizungumza kwa niaba  ya wenzao kwenye utambulisho wa mradi wa usawa na jinsia jana, walisema tangu mashirika na asasi za raia zianze kutoa elimu kuhusu haki za wanawake na watoto tabia za wake zao zimebadilika. Mmoja wa wanaume hao, Farijala Mchopa, alisema elimu inayotolewa na mashirika hayo inakwenda kinyume na imani ya dini zao na hivi sasa wanawake hao hawatawaliki kinyume na matakwa ya dini yao. Mchopa  alishauri asasi inayoratibu mafunzo hayo, Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto cha Lindi (LIWOPAC) na shirika la kimataifa la misaada la OXFA, kuhamasisha zaidi    watu wafunge ndoa za serikali  usawa unaohubiriwa uweze kukamilika na  kukubalika  kwa pande  zote. “Usawa huu ili ukubalike, mashirika haya yahamasishe kuanza mchakato wa kuanzisha vyama na mashirika ya kutetea haki za wanaume   na kuchangishana mahali,”alisema Mchopa. Msimamizi wa mradi huo, Romana Colman, licha ya kueleza lengo la mradi huo, alisema asasi za  iraia ikiwamo LIWOPAC hazina nia ya kufarakanisha jamii bali haki na usawa ndiyo msingi wa amani na utulivu katika jamii.
3
Na BENJAMIN MASESE -NANSIO MKUU wa Wilaya ya Ukerewe, Estomih Chang’ah, amesema hali ya usalama wa wilaya hiyo si shwari kutokana na   viasharia ambavyo vinaweza kusababisha maafa muda wowote. Alimwomba Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula kulifikisha suala hilo sehemu husika. Chang’ah alisema moja ya kiasharia cha kutokuwapo  usalama wa raia ni kivuko cha MV Nyerere ambacho hufanya safari zake kati ya Ukara na Bugorola Alisema kivuko hicho kimekuwa kikizua hofu mara kwa mara kutokana na kuharibikia katikati ya ziwa. “Kwa kuwa wilaya hii ipo kisiwani na baadhi ya wakazi wa Ukerewe   wanaishi katika visiwa vidogo vidogo, ninaweza kusema hali si shwari kwa baadhi ya wananchi hasa wanaosafiri au kusihi Ukara na Bugorola. “Naomba suala hili ulifikishe kwa wizara husika ili lifanyiwe kazi kwa uzito wake,” alisema. Alisema jambo la pili ambalo si zuri  ni vitendo vya watoto wa shule kupewa ujauzito. “Hapa Ukerewe mimba si za kuuliza.  Kibaya zaidi tunapofuatilia ipo tabia ya wazazi kushirikiana na watuhumiwa na kuyamaliza huko huko. “Tunashindwa kupata ushirikiano   kumkamata aliyempa mimba mtoto, isitoshe na hata mwanafunzi anakuwa hayupo tayari kumtaja. “Jambo hilo ni kubwa kwa kiasi chake ingawa vyombo vya dola vinapambana nalo… tunashindwa kufikia malengo ambayo tunayakusudia  yaani Ukerewe wanazaliana kweli kweli,” alisema. Naye  Waziri Mabula alisema suala la kivuko, katika bajeti ya 2017/2018, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, imekitengea fedha na aliahidi kulifikisha kwa waziri husika. Kuhusu mimba, alisema kwa mujibu wa sheria, mtuhumiwa anapaswa kwenda jela miaka 30. Aliomba uwepoa mpango wa kuangalia kufanya maboresho ya kuwahusisha wazazi wa wanafunzi ambao wanashindwa kutoa ushirikiano ili nao wajumuishwe katika adhabu ya miaka 30 jela. “Kuhusu uvuvi haramu, hili suala lipo katika Wilaya ya Ukerewe, Musoma na Ilemela, sasa ninachoomba ifanyike operesheni ya pamoja ambayo itahusisha vyombo vyote. “Maana tukifanya hapa Ukerewe watakimbilia kule Musoma au Ilemela, sasa tujipange ili msako ufanyike kwa pamoja katika wilaya zote,” alisema. Wakati huohuo, Naibu Waziri amemfuta cheo, Ofisa Ardhi Mteule wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe,  Eliah Mtakama  akidaiwa kuwa mzembe kazini na kushindwa kutimiza majukumu yake kwa  miaka 14. Vilevile, alimfuta cheo, Ofisa Ardhi Msaidizi wa Wilaya hiyo, Samwel Msungu, kabla ya kurejeshewa tena  baada ya kuwasilisha nyaraka  alizozitoa  wizarani akielezea changamoto ambazo zilimfanya kutotimiza majukumu yake ipasavyo ya kuingiza takwimu katika mfumo maalumu wa  utambuzi wa wamiliki wa viwanja na ulipaji kodi kwa miaka miwili mfululizo. Mabula alichukua hatua hiyo baada ya Mtakama kuwasilisha taarifa ya idara ya ardhi katika wilaya hiyo  huku ikiwa na upungufu mkubwa ambao ulisababisha kuongezeka migogoro  kati ya wananchi na serikali, taasisi za dini na mashirika binafsi na hakuna jitihada zilizowekwa kutatua kero hizo.
3
MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua mkoani Tabora, Dk John Pima ametunukiwa cheti maalumu cha utendaji uliotukuka kutokana na weledi wake wa kusimamia vizuri maendeleo ya halmashauri hiyo.Tuzo hiyo ilitolewa na Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo na kukabidhiwa kwake na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Tabora, Gullam Remtullah Dewji aliyekuwa mgeni rasmi katika baraza la jumuiya hiyo.Alipotafutwa na gazeti hili, Dk Pima amesema amepokea tuzo hiyo kwa furaha kubwa na kuahidi kuwa ataendelea kuwatumikia wananchi wote na kutoa ushirikiano mkubwa kwa jamii nzima.Ghullam alifafanua kuwa mtumishi yeyote anayepewa dhamana ya kutumikia jamii, akafanya kazi yake kwa weledi mkubwa na kwa moyo wa kupenda pasipo kutanguliza maslahi binafsi, anastahili kupongezwa.Alisema kuwa tuzo hiyo ni zawadi tosha ya kutambua mchango wake wa hali na mali, ambao umekuwa chachu ya kufanikisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za jumuiya na chama, ikiwemo maendeleo ya wananchi.“Dk Pima amekuwa msaada mkubwa sana kwa Jumuiya ya Wazazi na CCM kwa ujumla na ameleta mageuzi makubwa ya kiutendaji katika halmashauri anayoiongoza, tunampongeza sana,” alisema.Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wilayani humo, Haji Ally Kiyanga ‘Baggio’ alisema, mbali na kusaidia jumuiya za chama, Dk Pima amekabidhiwa tuzo hiyo kwa weledi wake mkubwa ambao umeifanya halmashauri hiyo kupaa kielimu.Alibainisha kuwa tangu ateuliwe kuwa mkurugenzi, halmashauri hiyo imepata mafanikio makubwa ikiwemo kushika nafasi ya kwanza kielimu katika mkoa wa Tabora na kuwa miongoni mwa halmashauri 10 bora nchini.Pia amewezesha halmashauri hiyo kuwa kinara wa ukusanyaji mapato kati ya halmashauri zote saba za mkoa huo, jambo ambalo limewezesha miradi mingi ya maendeleo kukamilishwa kwa kutumia fedha za ndani.
3
                                                                      Hadija Omary, Lindi Wakazi wa Wilaya ya Lindi, mkoani Lindi wamekusudia kumaliza tatizo la uchafu wilayani humo kwa kununua matela matano yenye thamani ya Sh milioni 60, yatakayotumika kama maeneo ya kukusanyia taka kwa sehemu zisizo na vizimba katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani humo. Akizungumza wakati hafla fupi ya uzinduzi wa matela hayo wilayani hapa, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shahibu Ndemanga pamoja na mambo mengine ameupongeza uongozi wa halmashauri hiyo ya kwa kuwa na mipango mizuri ya kuhakikisha manispaa inakuwa na vitendea kazi vya kisasa  vya kufanyia usafi. “Huwezi kukusanya taka wakati huwezi kuzizoa na kupeleka dampo huwezi kuwa na vifaa vya kuzolea taka wakati huna dampo, unakwenda kutupa wapi takataka? “Mmeamua kujenga dampo, mmenunua lori kwa ajili ya kubeba takataka mmenunua Kijiko kwa ajili ya kupakilia taka taka na leo mmenunua vizimba ambavyo vinatembea ni uamuzi mzuri na Manispaa tuendele kufanya hivyo,” amesema  Ndemanga. Aidha, Ndemanga pia ametoa wito kwa wananchi kuyatunza matela hayo dhidi ya uharibifu na hujuma mbali mbali zinazoweza kuzuilika kwani yatawekwa kwenye maeneo wanayoishi, ili yaweze kudumu kwa kutumika kwa muda mrefu. Awali akisoma taarifa ya ununuzi wa matela hayo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi,  Jomary Satura Afisa mazingira wa Halmashauri hiyo Vavenalis Mauna amesema matela hayo yana uwezo wa kubeba taka kati ya tani sita hadi saba kila moja na yana uwezo wa kumwaga taka yenyewe kwa kubinuka.  
0
“Hii ni dalili njema kwa uchumi wa nchi yetu na nchi jirani,” alisema Mkurugenzi wa kampuni inayojishughulisha na huduma za mizigo bandarini, Reindeer Investment Limited, Mlimuka Luhanga.Akizungumza mwishoni mwa wiki, Luhanga alisema juhudi za kuiimarisha Bandari ya Dar es Salaam zinaiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya ushindani katika eneo la Afrika na kama kazi hiyo ikifanywa vyema, itakuwa faida kubwa kwa wafanyabiashara wa ndani na nje pamoja na nchi kwa ujumla.Luhanga ameipa changamoto Serikali kuimarisha zaidi usafiri wa reli nchini, kwani utasaidia kwa kiasi kikubwa kusafirisha bidhaa zinazopakuliwa bandarini na kuzisafirisha sehemu husika.“Kwa kutumia barabara tu hatuwezi kufanikisha kusafirisha mizigo yote kwa wakati na vilevile barabara zetu hazitadumu kwa muda mrefu, tunahitaji miundombinu ya reli kwa kuwa itasaidia sana kusafirisha mizigo ndani na nje ya nchi jirani,” alisema Mkurugenzi huyo.Mdau mwingine, Safari Kazimoto ambaye anajishughulisha na shughuli ya uingizaji magari kutoka nje na kuyauza, amesifu maboresho ya huduma ya Bandari na kusema yamerudisha imani kubwa kwa watumiaji wa Bandari ya Dar es Salaam.“Kwa miezi ya karibuni biashara yangu imeimarika kutokana na ufanisi katika Bandari na vilevile msongamano umepungua na kuleta imani kwa watumiaji wa Bandari ya Dar es Salaam,” alisema Kazimoto.Mfanyabiashara kutoka Congo DRC, Pierre Nzwagiba, alisema Bandari ya Dar es Salaam ni kubwa na ina uwezo mkubwa wa kupitisha mizigo mingi na maboresho yaliyofanywa hivi karibuni yataimarisha biashara.“Naipongeza TPA kwa kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha imani ya watumiaji wa bandari hii wanarudi na wanaendelea kutumia huduma kama kawaida,” alisema Nzwagiba.Raia huyo wa Congo DRC, ameitaka Serikali kuendelea kuwekeza zaidi katika miundombinu na uboreshaji wa huduma bandarini na kutoridhika na maboresho hayo tu.Katika miaka ya hivi karibuni pamekuwepo mikakati mbalimbali inayofanywa na Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, TPA pamoja na wadau wengine, kuhakikisha bandari ya Dar es Salaam inatoa huduma bora kwa wateja wa hapa nchini pamoja na wale wa nchi jirani.Kutokana na mikakati hiyo, pamekuwepo na ongezeko la shehena na tija katika kuhudumia shehena na meli zinazotumia bandari hiyo na kupungua kwa msongamano wa meli.Pia kumekuwepo punguzo kubwa la mrundikano wa mizigo na kufanikiwa kukomesha vitendo vya upotevu wa mizigo na wizi kwa kiasi kikubwa.Kwa mfano, kwa upande wa mapato, mwaka 2012/13 wastani wa Sh bilioni 371.7 zilikusanywa, sawa na ongezeko la asilimia 14.3 ukilinganisha na Sh bilioni 325.3 mwaka 2011/12.Katika mapato hayo, bandari bila ya makusanyo ya TICTS, ilikusanya Sh bilioni 324.5 mwaka 2012/13, ikiwa ni ongezeko la asilimia 18.9, ikilinganishwa na mapato ya Sh bilioni 272.9 mwaka 2011/12.
5
PARIS, Ufaransa WATU  wapatao 1,726 walikamatwa na  polisi  kufuatia maandamano yaliyoikumba nchi hii  wiki iliyopita katika maeneo mbalimbali kupinga ongezeko  la kodi katika bidhaa mbalimbali hususan za mafuta. Taarifa  hiyo metolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Christophe Castaner  na akasema waandamanaji  1,220  waliwekwa rumande na wengine 619 wamshafunguliwa mashtaka. Waziri huyo alisema waandamanaji wengi walikutwa na silaha ingwa mawakili wao wanadai kuwa hawakuwa na vitu kama bali waliandamana kuonesha hisia zaoa kali na wala hawakufanya vurugu zozote. Waziri huyo alisema kuwa wengi wa waandamanaji ambao wanawashikilia mahabusu wanatuhumiwa kufanya vurugu ama kuhamasisha uharifu. Jumamosi hiyo ilishuhudiwa maandamano mengine ya nne yanayowahusisha watu wanaohitwa vizibao vya njano ambao wanapinga kuongezwa kwa bei ya mafuta, kodi na ghrama za maisha. Katika jiji hili la Paris, Lille, Lyon, Marseille, Nantes  na  Toulouse waandamanaji hao walipambana na polisi na kati yao  135 walijruhiwa mjini hapa. Maandamano hayo yalianza baada ya Novemba 17 mwaka huu serikali kutangaza kuwa bei yha mafuta ya petroli  na dizeli nchini itapanda kuanzia  Januari mosi  mwakani senti Euro 3  kwa petrol na senti Euro  6.5 kwa dizeli.
2
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam MWIMBAJI wa muziki wa injili, Emmanuel Mbasha, anayekabiliwa na kesi ya kumbaka mtoto wa miaka 17, jana alitoka kwenye chumba cha Mahakama ya Wilaya ya Ilala akibubujikwa machozi. Hali hiyo ilimtokea mara baada ya shahidi wa pili wa kesi hiyo, aliyejulikana kwa jina la Suzan, kutoa ushahidi wake. Kwa kuwa kesi hiyo inasikilizwa kwenye chemba (chumba maalumu ambacho waandishi na watu wasiohusika hawaruhusiwi kuingia) haikuweza kujulikana mara moja ni kitu gani kilichofanya mwimbaji huyo ambaye kwa sasa ameachana na mkewe, Flora Mbasha alie. Mara baada ya kesi hiyo kuahirishwa na Mbasha kuondoka kwenye viwanja vya mahakama hiyo akiwa na wakili wake, Ngassa Ganja, Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga, alisema shahidi huyo aliieleza mahakama jinsi binti anayedaiwa kubakwa alivyomsimulia namna alivyotendewa kitendo hicho. Alisema shahidi huyo alitoa ushahidi wake mbele ya hakimu Flora Mjaya. “Mnakumbuka ile siku ambayo shahidi namba moja (binti aliyebakwa) alivyoieleza mahakama kwamba walikwenda kwa dada yake kumtafuta Flora ndipo akabakwa na Mbasha? Basi huyu shahidi namba mbili (Suzy) ndiye yule dada yake,” alifafanua. Katuga alisema shahidi huyo aliieleza mahakama kuwa alipata taarifa zote hizo baada ya binti anayedaiwa kubakwa kukimbilia nyumbani kwake na kumpa taarifa zote. “Lakini kwa mujibu wa sheria (CPA) namba 186 kifungu kidogo cha tatu, inanizuia kueleza kwa kina yale ambayo shahidi huyo ameieleza mahakama,” alidai Katuga. Kwa upande wake, wakili wa Mbasha, Ganja, aliliambia MTANZANIA kuwa licha ya shahidi huyo kueleza kwamba binti anayedaiwa kubakwa alipigwa na Mbasha, yeye shahidi hakumkagua ili kujiridhisha kama ni kweli alipigwa ama la. “Ni kweli ameieleza mahakama ushahidi ambao Katuga amewaeleza, ila shahidi huyo hakumkagua (binti aliyebakwa) ili kujua kama ni kweli,” aliongeza. Mbasha alifika mahakamani hapo mapema saa tatu asubuhi. Hata hivyo kesi hiyo iliahirishwa kwa muda kutokana na wakili wake, Ganja kuchelewa kufika mahakamani hapo. Ilipofika saa tano, kesi hiyo iliitwa tena na ushahidi huo kusikilizwa kwa takriban saa mbili, mbele ya hakimu Mjaya. Katika kesi hiyo Mbasha ambaye ni mume wa mwimbaji maarufu wa muziki wa injili, Flora Mbasha, anadaiwa kumbaka shemeji yake mwenye umri wa miaka 17, kati ya Mei 23 na 25 mwaka jana eneo la Tabata ambako alikuwa akiishi naye. Septemba 5 mwaka jana, binti huyo aliieleza mahakama kuwa alibakwa na shemeji yake huyo kwa awamu mbili tofauti kabla ya kufanikiwa kukimbia. Kesi hiyo inasikilizwa mahakamani kwa siri kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ya mwaka 2003 sura ya 20 kifungu cha 186, kifungu kidogo cha tatu ili kulinda haki ya binti huyo.
1
SHIRIKA la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) limefanya ziara ya siku moja ya ukaguzi wa ukarabati wa meli za MV Victoria na MV Butiama na kuridhishwa na maendeleo yake. Akizungumza wakati wa ziara hiyo ya siku moja mkoani hapa, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TASAC, Profesa Thadeo Satta, alisema wamefanya ziara hiyo kutokana na kazi yao kubwa ni udhibiti wa usalama wa vyombo vya majani. Alisema wamepewa matumaini makubwa na msimamizi wa mradi wa ukarabati wa meli hizo, Abel Gwanafio, kuwa meli hizo zitamalazika kwa wakati ambao ni mwisho wa Machi mwakani. Profesa Satta alisema kwa sasa TASAC wapo katika mkakati mkubwa wa kutengeneza mifumo ya teknolojia ya kielektroniki ya kudhibiti uzito wa mizigo, idadi ya abiria pamoja na tiketi zinazotolewa na usalama wa vyombo usafiri majini. Alisema mpaka sasa ukarabati wa Mv Victoria umefikia asilimia 37 na wa Mv Butiama umefikia asilimia 22.5. Alisema ukarabati wa MV Victoria utagharimu Sh bilioni 22 na meli hiyo itawekwa injini mbili mpya na majenereta makubwa matatu, huku MV Butiama ikigharimu Sh bilioni nne na itawekwa mitambo saidizi mipya.
3
 NORA DAMIAN -DAR ES SALAAM MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesema katika mwaka wa fedha wa 2018/19 halmashauri nchini zilikusanya Sh bilioni 300 kati ya Sh bilioni 736 zilizopangwa kukusanywa. Kiasi hicho ni chini ya asilimia 50 ya mapato yaliyokusudiwa huku zaidi ya asilimia 70 ya halmashauri zikishindwa kufanikisha malengo yake ya kila mwaka ya ukusanyaji mapato ya ndani. Aidha katika mwaka 2017/18 halmashauri zilipanga kukusanya Sh bilioni 687 na kufanikiwa kukusanya Sh bilioni 281 tu ambazo ni sawa na asilimia 41 ya lengo lililowekwa. Kichere amebainisha hayo kupitia ripoti ya ukaguzi wa ufanisi kuhusu ukusanyaji mapato toka vyanzo vya ndani katika mamlaka za Serikali za mitaa. Ukaguzi huo ulijumuisha miaka minne ya fedha kuanzia 2015/16 hadi 2018/19 ambapo timu ya ukaguzi ilichagua mikoa sita ya Iringa, Kigoma, Mwanza, Dodoma, Mtwara na Dar es Salaam wakati halmashauri ni Kinondoni MC, Kigamboni DC, Dodoma CC, Chemba DC, Iringa MC, Iringa DC, Kasulu TC, Kigoma DC, Mwanza CC, Sengerema DC, Mtwara MC na Masasi DC. “Ukaguzi ulichochewa na matatizo ya kiutendaji ya halmashauri katika ukusanyaji wa mapato,” alisema Kichere. HALMASHAURI Ukaguzi huo ulibaini kwa miaka minne ya fedha kuanzia 2015/16 hadi 2018/19, karibu asilimia 70 ya halmashauri hazikufanikisha malengo yao ya ukusanyaji mapato.  “Mahitaji ya rasilimali za kifedha ya kukidhi huduma tofauti za kijamii katika mamlaka za Serikali za mitaa yamekuwa yakiongezeka, mchango wa mapato unaendelea kupungua kutoka asilimia 28 mwaka 2015/16 hadi asilimia asilimia 11 mwaka 2018/19.  “Hali hii inamaanisha kuwa Serikali inaingiza sehemu kubwa ya fedha kwenye bajeti za halmashauri kinyume na malengo ya kupunguza utegemezi wa ufadhili wa Serikali Kuu,” alisema Kichere. SABABU Katika ukaguzi huo, Kichere alisema mamlaka za Serikali za mitaa hazifanikishi malengo yaliyowekwa ya ukusanyaji wa mapato kutoka katika vyanzo vyake kwa sababu hazijiwekei malengo halisi ya ukusanyaji.  “Kwa wastani zaidi ya asilimia 53 ya halmashauri zilirekodi tofauti zaidi ya asilimia 20 kutoka malengo yaliyowekwa licha ya msisitizo uliowekwa na Serikali kwamba tofauti katika malengo yaliyowekwa hayapaswi kuzidi asilimia 20 kwa kila chanzo cha mapato,” alisema Kichere. Kulingana na ripoti hiyo, sababu zingine ni pamoja na usimamizi duni, ukosefu wa mikakati madhubuti ya kupanua wigo wa ushuru katika halmashauri na upungufu wa watumishi kati ya asilimia 23 na 70 katika idara za fedha na biashara. “Maofisa wachache waliokuwepo walikosa ujuzi wa kutosha wa makadirio ya mapato na kukagua kodi kwa vyanzo vya mapato kama vile ushuru wa hoteli na ushuru wa huduma. “Maofisa hawakuwa na maarifa ya kutosha na uwezo wa kutosha kuendesha mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia za kielektroniki (LGRCIS) na mashine za kukusanya mapato (PoS),” alisema Kichere. Alisema pia kukosekana kwa mafunzo ya mara kwa mara na kucheleweshwa kwa mawasiliano ya mabadiliko katika mifumo ya ukusanyaji wa mapato kulisababisha pengo la maarifa kwa watumiaji wa mifumo. Kichere alisema mifumo ya ukusanyaji wa mapato haikuunganishwa vizuri na akaunti kadhaa za benki na kusababisha utengamano kati ya ripoti za mapato zinazotokana na mifumo hiyo na zile zinazotokana na benki. SHERIA ZILIZOPITWA NA WAKATI Ukaguzi ulibaini kuwa halmashauri saba kati ya 12 zilizotembelewa zilikuwa zikitumia sheria ndogondogo ambazo hazikupitiwa upya kuzioanisha na viwango vya sasa vya soko, hususan ada na ushuru unaokusanywa kutoka kwenye masoko. Kulingana na ripoti hiyo, katika halmashauri tatu zilizotembelewa takribani Sh milioni 104.2 hazikukusanywa kwa mwezi kwa sababu ya matumizi ya bei ambayo yalikuwa chini kuliko bei ya soko. “Kutotekelezwa kwa sheria ndogo ndogo zinazopitishwa na mabaraza ya halmashauri ni kati ya sababu, maofisa waliohojiwa pia walionyesha kuwa kuna kuchelewa kupata idhini kutoka serikalini kwa sheria ndogo ambazo wakati mwingine huchukua hadi miezi sita. “Kumesababisha kutoboreshwa kwa ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo vilivyopo kwa sababu ya matumizi ya viwango vya zamani,” alisema Kichere.  WAKUSANYA USHURU Ukaguzi ulibaini pia mamlaka ya Serikali za mitaa hazikuwasimamia vyema wakusanya ushuru katika maeneo yao.  “Wakusanya ushuru walikuwa wanakosa zana za ukusanyaji wa mapato na uwezo wa kutosha kuwawezesha kutumia mifumo ya ukusanyaji wa mapato na vifaa. Hii ilisababisha kuongezeka kwa makosa. “Ukaguzi ulibaini kuwa halmashauri hazikufanya tathmini ya utekelezaji wa mikataba ya mawakala wa kukusanya mapato kama ilivyoainishwa katika mwongozo wa wakala wa kukusanya mapato ya nje ya mwaka wa 2016.  “Halmashauri hazikuchukua hatua sahihi za marekebisho kwa wakusanya ushuru ambao hawakuzingatia masharti ya mikataba yao,” alisema Kichere. Alisema hata ripoti za uchunguzi wa Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2015/16 hadi 2018/19 katika idara za fedha za halmashauri na sekretarieti za mkoa hazikuwa zikitoa taarifa kamili na za kina juu ya utendaji wa ukusanyaji wa mapato katika halmashauri, badala yake zina muhtasari wa mafanikio ya malengo ya jumla ya ukusanyaji wa mapato. MAPENDEKEZO Kichere alishauri Serikali itathmini ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato na kushughulikia makosa yote ili kuhakikisha mifumo inafanya kazi vizuri. “Mfumo lazima pia uweze kuonyesha kwa usahihi na kwa wakati mapato yaliyokusanywa na kuweza kutoa ripoti zinazohitajika kwa ajili ya kufanya maamuzi. “Halmashauri ziwe na mipango madhubuti ya ukusanyaji wa mapato ambayo pia itahusisha mapitio ya mara kwa mara ya sheria ndogo, zikague mara kwa mara utendaji wa wakusanya ushuru katika maeneo yao na kuchukua hatua za haraka kurekebisha mapungufu,” alisema Kichere.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amezitaka halmashauri kuwawezesha vijana mikopo ya asilimia 4 ya mapato ya ndani wanayotenga kwa ajili ya kuwawezesha vijana kujenga Vitalu Nyumba (Green House) vyao binafsi. Ametoa kauli hiyo juzi wakati wa Uzinduzi wa Mafunzo kwa Vijana ya Kilimo cha Kisasa kwa kutumia teknolojia ya Kitalu Nyumba katika Viwanja vya Nanenane, Ngongo Mkoani Lindi. Waziri Mkuu amesema vijana ni rasilimali muhimu katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo katika jamii, hivyo Rais John Magufuli aliamua kuwajengea vijana mazingira wezeshi ikiwemo kupata fursa za mikopo na ujuzi unahitajika ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za kimaendeleo. Alieleza kuwa, Serikali iliamua kuanzisha utaratibu wa kila halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa lengo la kutoa mikopo isiyo na riba kwa vijana asilimia 4, wanawake asilimia 4 na wenye ulemavu asilimia 2. “Halmashauri zote zihakikishe zinatenga kiasi cha fedha kwa ajili ya kuwawezesha vijana ili waweze kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo shughuli za kilimo zitakazowasaidia kujiajiri na kujiingizia kipato,”alisema.Alifafanua kuwa sekta ya kilimo ndiyo kimbilio la wananchi wengi na kwa kutumia teknolojia ya kitalu nyumba vijana wengi watapata ajira katika sekta hiyo kwa kuwa ina faida kubwa sana ikiwemo kupata mazao mengi katika eneo dogo na kupata mazao bora yanayokidhi viwango katika soko la ndani nan je ya nchi. Waziri Mkuu aliongeza kuwa Serikali kupitia Ofisi yake imeendelea kuratibu programu ya ukuzaji ujuzi nchini na imeanza kutoa mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa kutumia teknolojia ya Kitalu Nyumba katika Mikoa yote na Halmashauri zote nchini.
3
JESHI la Polisi mkoani Katavi limetumia mabomu kuwatawanya waumini wenye hasira waliovamia na kushambulia kwa mawe nyumba ya mchungaji wa Kanisa la Sauti ya Uzima na Uponyaji, Nabii Elia (36) wakimtuhumu kuwa ni mshirikina.Jina kamili la Nabii Elia limeelizwa kuwa ni Elia Zabron Balashika na inadaiwa kwamba ni raia wa Burundi na kwamba amekuwa akitoa huduma ya kiroho kwa zaidi ya miaka sita sasa.Ndugu wawili wa Nabii Elia, Musa Elia (24) ambaye pia ni mchungaji wa kanisa hilo na mkazi wa Mtaa wa Kazima na muumini wa kanisa hilo Joseph Elia (29) mkazi wa Mtaa wa Tulieni- Kazima wamejeruhiwa kwa kupigwa na mawe.Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi , Damas Nyanda ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea Mtaa wa Kazima Ringini katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi ambapo waumini watano wa kanisa hilo huku wengine wakiwa sio waumini wa kanisa hilo wamekamatwa kwa kosa la kujichukulia sheria mkononi na kuharibu mali ya Nabii Elia .Aliwataja waumini wa kanisa hilo waliokamatwa kuwa ni pamoja na William Kaluzi (19) mkazi wa Mtaa wa Nsemulwa , Steven Alfred (31) mkazi wa Mtaa Kazima , Nicholaus Shadrack (33) mkazi wa Mtaa wa Kazima na Tekla Didas (17) mkazi wa kijiji cha Rungwa Wengine ambao sio waumini wa kanisa hilo ni pamoja na Mashaka Moshi (23) mkazi waMtaa wa Nsemulwa na Fraja Hussein (22) mkazi wa Mtaa wa Kazima.Kamanda Nyanda amesema kuwa chanzo cha vurugu hizo ni imani za kishirikina baada ya taarifa kuzagaa kuwa Nabii Elia alikuwa ameweka 'misukule' watano nyumbani kwake.Aliongeza kuwa siku hiyo ya tukio saa 11.30 jioni , Nabii Elia alifika katika Kituo cha Polisi mjini Mpanda ambapo alitoa taarifa kuwa amevamiwa nyumbani kwake mtaa wa Kazima na wananchi wenye hasira wakiwa na mawe na kuharibu mali zake."Ndipo timu ya askari polisi wakiongozwa na SSP Focus Malengo , Mkuu wa Upelelezi (Jinai) mkoa wa Katavi Abdallah Hussein na Kaimu Ofisa Upelelezi wa wilaya ya Mpanda , Mkaguzi Ngagala walifika eneo la tukio na kukuta kundi la wananachi wenye hasira wakiendelea kurusha mawe " alielezaAliongeza kuwa katika kutuliza ghasia mabomu matatu ya kishindo yalitumika kuwatawanya wananchi hao ambapo waumini wawili wa kanisa hilo walijeruhiwa kwa kupigwa mawe kichwani.Walijeruhiwa ni pamoja na Mussa Elia (24) ambaye ni mchungaji wa kanisa hilo na Joseph Elia (29) mkazi wa Mtaa wa Kazima ambaye ni muumini wa kanisa hilo wote wameeleza kuwa ni ndugu wa Nabii Elia.Kamanda Nyanda akifafanua alisema kuwa mali za Nabii Elia zilizoharibiwa ni pamoja na vioo vinne vya madirisha ya nyumba yake , kioo cha nyuma cha gari lake aina ya Spacio huku thamani kamili haijaweza kufahamika mara moja .
3
Simba na Yanga zinatarajiwa kumenyana Jumapili hii kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam katika mechi ya raundi ya pili ya Ligi Kuu Bara.Ninja, ambaye katika mechi za hivi karibuni amekuwa akicheza kwa kiwango kikubwa, aliliambia gazeti hili jana kuwa kukutana na Simba kwake si mara ya kwanza hivyo anaifahamu presha ya kucheza na timu hiyo lakini zaidi hawahofii washambuliaji tishio kwa sasa wa wapinzani wao hao na akaapa kuwadhibiti kikamilifu.“Nilishawahi kukutana na Simba mara mbili nikiwa Taifa Jang’ombe katika michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa hiyo si mara yangu ya kwanza kucheza na timu hiyo, nawajua vizuri lakini pia mimi siwahofii nawaona kama ni wachezaji wa timu nyingine tu.“Kweli wanaongoza kwa kufunga msimu huu, lakini mimi nimejipanga vya kutosha ukichanganya na mbinu ninazopewa na makocha wangu katika mechi hiyo naamini hawatakuwa na madhara, tusubiri tu siku ya mechi,” alisema Ninja.Upande wa Simba, Bocco mwenye mabao 14 na Okwi mwenye 19 wakiwa vinara wa kufumania nyavu mpaka sasa wanaonekana tishio kwa ukuta wa Yanga kutokana na spidi yao, lakini Simba pia watakuwa na shughuli pevu ya kuwazuia Obrey Chirwa na kinda Yusuf Mhilu anayeonekana kufanya vizuri zaidi kila anapopata nafasi katika mechi za hivi karibuni.
4
WASHAMBULIAJI wa Simba huenda wakakutana na nafuu baada ya wapinzani wao Al-Ahly kuthibitisha kumkosa beki wao tegemeo, Saad Samir ambaye alimdhibiti vilivyo Meddie Kagere katika mchezo uliofanyika nchini Misri wiki moja iliyopita.Msafara wa mabingwa hao wa zamani wa Afrika uliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jana bila ya beki huyo aliyewadhibiti vilivyo washambuliaji wa Simba wakiongozwa na Meddie Kagere kwenye mchezo ambao Simba walifungwa mabao 5-0.Saad Amir ni beki mwenye uzoefu wa mashindano mbalimbali aliwahi kucheza mechi za kufuzu Kombe la Dunia kwa miaka kadhaa na Kombe la Mataifa ya Afrika na amekuwa akitegemewa katika idara ya ulinzi ya timu hiyo kutokana na uwezo wake wa kukaba na kupandisha mashambulizi.Mabingwa hao wa kihistoria wa Ligi ya Mabingwa Afrika wanaongoza katika kundi D wakiwa na pointi saba, wakifuatiwa na As Vital wenye pointi 4, Simba ina pointi tatu na Js Saoura ikiwa na pointi mbili baada ya kutoa sare michezo miwili na kupoteza dhidi ya Simba.
4
MWANAFUNZI Mtanzania Allen Buberwa (22) aliyekuwa akisoma chuo nchini Marekani, ameripotiwa kufa maji katika mto Buffalo uliopo Pruitt Jimbo la Arkansas.Taarifa za Serikali ya Jimbo la Arkansas, imethibitisha tukio hilo na kueleza kuwa Buberwa aliyekuwa akisoma Chuo cha North Arkansas katika Mji wa Newton, alifikwa na umauti Jumatatu jioni wiki hii baada ya kuzama kwenye kina kirefu cha mto huo.Taarifa hiyo ya serikali imefafanua kuwa Buberwa, alikuwa akiogelea katika eneo maarufu la kuogelea kabla ya kuzama katika kina kirefu na kufa.Wazamiaji waliupata mwili wa Buberwa Jumatatu hiyo saa tano usiku (kwa muda wa Marekani). Alikuwa katika programu ya wanafunzi wa Kimataifa katika chuo hicho.Mamlaka zilipewa taarifa ya tukio hilo saa 12 jioni (kwa saa za Marekani) wakati Buberwa na watu wengine watatu walipoonekana wakijaribu kuogelea katika mto huo kuelekea katika eneo jingine la mto. Taarifa ya serikali inasema Buberwa alionekana kuogelea kwa tabu na alifika eneo lenye kina kirefu na alipozama ndani ya maji, hakuibuka tena.“Waogeleaji wenzake hawakufanikiwa kumuokoa,” ilieleza taarifa hiyo.Kwa mujibu wa taarifa ya Serikali ya Newton iliyotolewa na kiongozi wa eneo hilo, Glenn Wheeler, maofisa wa serikali walielezwa na mashuhuda kuwa Buberwa aliteleza na kutumbukia katika mto huo kwenye eneo la kina kirefu na mtu mmoja alipiga mbizi kumuokoa, lakini wote walionekana kuhangaika kujiokoa.“Hata hivyo, mashuhuda wametueleza kuwa watu wawili walizamia kwenye maji na kufanikiwa kumuokoa yule mti alutejitupa ili kumuokoa Buberwa na Buberwa alipotelea majini na mwili wake uliibuliwa saa tano baada ya kuzama,” alisema Wheeler katika taraifa yake.“Tukio hili ni baya na la kuhuzunisha, tunaiombea familia yake na marafiki,” alisema Wheeler na kuongeza kuwa, tukio hilo limekatisha ndoto ya kijana huyo mdogo aliyekuwa akisoma katika Chuo cha North Arkansas karibu na Harrison.Mwakilishi wa chuo alichokuwa akisoma mwanafunzi huyo alikuwa eneo la tukio kushiriki kumtafuta na alikuwa akiwasiliana na familia ya Buberwa iliyopo nchini Marekani na Tanzania.Wheeler alisema waokoaji kutoka Ofisi ya Newton, Huduma za Hifadhi za Jamii, BUFFSAR, Kitengo cha Majanga cha Mennonite, taasisi za kidini, Kitengo cha Zimamoto na Uokoaji cha Harrison, Kituo cha Afya cha Arkansas (EMS), Kikosi cha Msalaba Mwekundu cha America na vikosi vingine vya zimamoto kutoka maeneo mbali mbali walishiriki kutafuta mwili wa Buberwa.Mto huo upo umbali wa kilometa 169 kaskazini magharibi mwa mji maarufu wa Little Rock.Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilipoulizwa jana kuhusu tukio hilo, ilisema inafuatilia kupata uhakika wake na itaujulisha umma wa Watanzania.
3
Klabu ya soka ya Yanga imefanikiwa kutinga kwenye hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho la Azam baada ya kuifunga Kagera Sugar kwa goli 2-1 kwenye mchezo ulipingwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Yanga ambayo inatinga kwa mara ya tano mfululizo kwenye hatua ya nusu fainali imefanikiwa kufika hatua kupitia kwa magoli ya David Molinga na Deus Kaseke Yanga sasa inasubiri mshindi wa mchezo wa pili wa robo fainali kati ya Simba na Azam unaotarjiwa kucheza hapo kesho ili kucheza naye kwenye hatua inayofuata ya kombe hilo Yanga inakua timu ya pili kufuzu kwenye hatua hiyo baada ya Namungo FC ya Lindi kufanya hivyo kwenye mchezo wa awali uliopigwa mapema leo Juni 30,2020 kwenye uwanja wa Kassim Majaliwa mjini Ruagwa.   FULL TIME | Yanga wanatinga nusu fainali #ASFC FT: Yanga SC 2-1 Kagera Sugar. Weka maoni yako hapa.#AzamSports2 #ASFC #AzamSportsFederationCup #KombeLaShirikisho #ASFC #YangaSC #KageraSugar #YangaKagera pic.twitter.com/b2wMBNnYgh — Azam TV (@azamtvtz) June 30, 2020
4
Hicho kilikuwa kilio kikubwa kwa klabu za ligi, hasa Yanga, Azam na Simba, ambazo ndizo zinazosajili wachezaji wengi wa kigeni. Kabla ya TFF kupitisha uamuzi huo, klabu ziliruhusiwa kusajili wachezaji watano tu wa kigeni.Habari kutoka ndani ya kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika mjini hapa jana zilisema kuwa, mvutano ulikuwa mkali wa ama kusajili wachezaji watano au saba.“Mjadala ulichukua muda mrefu sana, lakini kama unavyojua hiki kitu klabu kubwa zina maslahi nacho, na ndio waliotoa ushawishi kwa wajumbe wengi kutaka usajili wa wachezaji saba… mwisho tukakubaliana hivyo na hao saba wanaruhusiwa kucheza wote kwenye mechi moja,” alisema mtoa habari wetu kutoka ndani ya kikao hicho.Habari zaidi kutoka ndani ya kikao hicho zilisema, kuna masharti mengi klabu zimewekewa kama zinataka kusajili wachezaji hao saba. “Tumeweka masharti magumu lakini baadhi ni lazima kila mchezaji alipiwe ada ya dola za Marekani 2,000 kwa mwaka…“Lakini pia mchezaji anayesajiliwa kutoka nje lazima awe anacheza timu ya taifa ya nchi husika au Ligi Kuu,” kilisema chanzo chetu hicho.Hii si mara ya kwanza kwa klabu za Ligi Kuu kuruhusiwa kusajili wachezaji zaidi ya watano, miaka ya nyuma ilikuwa ikisajili wachezaji 10 na kuruhusiwa kutumia watano kwenye mechi moja, lakini hakukuwa na masharti yoyote ya aina ya wachezaji wa kusajiliwa, hali iliyofanya klabu kusajili wachezaji wasio na uwezo, ama majeruhi ambao wakifika nchini hushindwa kutoa msaada kwa klabu husika.Mwaka 2007 kulifanyika kongamano Bagamayo, ambapo baadhi ya maazimio kwenye kongamano lile ni kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni ambapo ilikubalika mpaka msimu uliopita klabu zisajili wageni watano na watakaotumika kwa mechi moja wawe watatu tu.Lakini hali imekuwa tofauti baada ya baadhi ya klabu kudai kuongezewa idadi ya usajili wa wachezaji wa kigeni ili zifanye vizuri kwenye michuano ya kimataifa.Hata hivyo, TFF hushindwa kufuatilia kanuni zake ambapo kuna wakati ilisema mchezaji wa kigeni awemo katika timu ya taifa lakini, lakini hilo walishindwa kulifuatilia na ni wachezaji wachache tu waliofikia kigezo hicho.
4
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameamuru kufungwa kwa masoko yote, yanayotumika kwa pamoja baina ya wakimbizi na Watanzania, yaliyopo kwenye vijiji kuzunguka makambi hayo ya wakimbizi.Ameeleza kuwa masoko hayo yamekuwa chanzo kikubwa cha kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu na ujambazi wa kutumia silaha mkoani Kigoma. Waziri Mkuu alisema hayo kwenye kikao na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya Kibondo mjini Kigoma jana. Alisema kuwa taarifa zinabainisha kuwa masoko hayo ni chanzo kikubwa cha uhalifu kwa wakimbizi kutoroka kambini na kuingia mtaani.Badala yake, alitaka masoko hayo yajengwe ndani ya makambi ya wakimbizi na kuwekwa utaratibu maalumu wa vibali maalumu vya wananchi wanaoishi vijiji kuzunguka makambi hayo kuingia kambini kufanya biashara au kununua bidhaa kutoka kwenye masoko hayo. Alisema kuwa pamoja na masoko hayo kuwa nje ya makambi ya wakimbizi, pia upo udhaifu mkubwa wa watendaji katika kudhibiti wakimbizi wanaotoka kambini bila utaratibu.Wakimbizi hao wamekuwa ndiyo chanzo cha vitendo vya uhalifu, huku silaha kubwa za kivita zikiwemo bunduki aina ya AK47, RPV, LMG ambazo si rahisi kwa walinzi wetu wa kawaida kuwa nazo zikitumika. Kutokana na hali hiyo, Majaliwa alisema kuwa ni lazima masoko hayo yafungwe na kufuata utaratibu mwingine, kwani serikali haitaki kuona uhusiano wa Tanzania na Burundi unavurugika, chanzo kikiwa ni masoko hayo.Akizungumza mbele ya Waziri Mkuu kwenye mkutano huo, Mkuu wa Wilaya Kibondo, Loius Bura alimweleza Waziri Mkuu kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, imebaini kuwa uwepo wa masoko hayo ni moja ya vyanzo vya ongezeko la vitendo vya uhalifu na wakimbizi kutoroka kambini na kuingia mtaani.Katika mkutano huo, Waziri Mkuu alipiga marufuku kwa mtu yeyote kuvaa nguo zinazofanana na sare za jeshi, zilizokamatwa kwenye kambi za wakimbizi za Nduta Wilaya ya Kibondo na Mtendeli, wilaya ya Kakonko zikigawiwa kwa wakimbizi. Alisema kuwa ni marufuku kwa mtanzania yeyote, kukutwa amevaa sare hizo za jeshi, kwani taarifa alizonazo zinaeleza kuwa karibu sare 300 ziligawanywa kwa wananchi mjini Kibondo. Hivyo, aliwataka wananchi walio na sare hizo, kuziwasilisha kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.Akitoa taarifa kwa Waziri Mkuu kwenye mkutano huo, Kaimu Mkuu wa Makazi katika Kambi ya Wakimbizi ya Nduta Wilaya ya Kibondo, Barnabas Kipi alisema kuwa wakimbizi 250 wamekamatwa mtaani wilayani Kibondo tangu mwezi Januari mwaka huu kwa kutoroka.Alisema tayari hatua mbalimbali za kisheria dhidi ya wakimbizi hao zimechukuliwa. Waziri Mkuu akizungumza na wananchi wa mjini Kakonko, aliwataka wananchi hao kuwa walinzi wa nchi yao na kuwafichua wakimbizi wanaoishi kwenye maeneo yao isivyo halali. Alisema wakimbizi watabaki kuwa wakimbizi na sheria na taratibu za kuwahifadhi wakimbizi, zitafuatwa.
3
Na Asha Bani -Dar es salaam MKUU wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro, amesema tatizo ndani ya jeshi hilo ni unafiki na kusisitiza mwenye wadhifa alionao yupo mmoja tu. Hayo aliyasema jana wakati akifungua kikao kazi kwa makamishna, makamanda wa mikoa, vikosi na maofisa waandamizi wa Jeshi la Polisi, Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay, Dar es Salaam. Alisema ana muda mchache wa kukaa katika kiti hicho, hivyo  wale wanaoona hafai nafasi hiyo wasubiri kidogo kwani wakati wao ukifika na wao wataweza kuchukua madaraka mbalimbali ndani ya jeshi hilo. “Tatizo linalotusumbua sisi Jeshi la Polisi pia ni unafiki. ‘There is no way’ tukawa na IGP zaidi ya mmoja, mimi sikujichagua. “Kamanda wa Kinondoni unanisikia (Mussa Taibu)? Kubali yaishe, sikujiteua mwenyewe, siwezi kujiona kama sitoshi katika nafasi hii. “Natamani kumaliza nafasi yangu Jeshi la Polisi likiwa na heshima yake. Jeshi hili likiharibika tumeharibikiwa wote, na mimi siwezi kumuwekea mtu kinyongo, mie sio wa aina hiyo, kwa hiyo niwaombe ushirikiano,” alisema IGP Sirro. Alipoulizwa kuhusu kauli ya IGP Sirro, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Taibu, alisema kuwa anafikiri kwamba alitumia jina lake kama njia ya kufikisha ujumbe kwa watu waliorushiwa kombora hilo. “Hakika hii ni nondo kwa watu waliopigwa hapa, na kunitaja mimi ilikuwa ni njia tu ya kufikisha ujumbe kwa baadhi ya watu. Na ujumbe kwao umefika vema,” alisema Kamanda Taibu. IGP Sirro aliteuliwa Mei 28, mwaka juzi kushika wadhifa huo, akichukua nafasi ya Ernest Mangu aliyeteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda. “Sina ubaya na askari yeyote na najua nikimuwekea mtu kinyongo nitakosa raha kwani hii ni kazi ya utumishi wa umma, leo nipo kesho sipo, kinachotakiwa ni kufuata mwongozo na utekelezaji wa kanuni za Jeshi la Polisi,” alisema IGP Sirro. Mbali na hayo, IGP Sirro alisema bado jeshi hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kumomonyoka maadili katika utendaji wa kazi pamoja na kudhoofu kwa utekelezaji wa  mpango mkakati wa jeshi la polisi. UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA Akizungumzia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24, IGP Sirro aliwataka askari polisi kuongeza umakini katika utendaji wao wa kazi kuelekea uchaguzi huo. Hata hivyo alikumbusha vifo vya aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), Akwilina Akwiline aliyeuawa Februari 17, mwaka jana wakati wa maandamano ya wafuasi wa Chadema kwenda kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni kudai viapo vya mawakala. Katika maandamano hayo inaelezwa kuwa polisi walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya mamia ya wafuasi wa chama hicho waliokuwa wakiandamana. Mbali na hilo, pia IGP Sirro alizungumzia kifo cha mwanahabari Daudi Mwangosi, ambaye alifariki dunia kwa kulipuliwa na bomu Septemba 2, 2012 katika Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi alipokuwa akitekeleza majukumu yake ya kazi wakati wa ufunguzi wa tawi la Chadema.  “Mkutano huu utakuwa ni kujipanga kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Ndugu zangu mtakumbuka kesi ya Akwilina na Mwangosi. “Sasa tunakwenda katika uchaguzi, hauwezi kupuuza, ili uweze kwenda vizuri lazima kuwa na mpango mkakati wa kuzuia na kupambana na wale watakaoleta uhalifu wa kuvuruga,” alisema IGP Sirro. Alisema katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Jeshi la Polisi linafanya kazi zake kwa umakini zaidi ikiwa pamoja na kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama na amani iliyopo inaendelea kudumu. RUSHWA POLISI IGP Sirro aliwataka makamanda wa polisi wa mikoa na vikosi vya jeshi hilo kujiepusha na vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu pamoja na kushiriki kikamilifu kuunga mkono jitihada za Serikali kufanikisha Tanzania ya viwanda. Alisema wapo baadhi yao wachafua sifa ya jeshi hilo jambo ambalo ni lazima lipingwe ili kuendelea kulinda hadhi yao. IGP Sirro alisema lazima Jeshi la Polisi liendelee kulinda usalama wa raia na mali zao na hatarajii kuona linakuwa chanzo cha migogoro kati yake na wananchi. “Kuna baadhi ya askari polisi bado wanaendeleza vitendo vinavyoashiria kuomba rushwa kwa wenye kutenda makosa na hasa barabarani. “Jeshi la Polisi halitaki kuona rushwa kwa watumishi wake na hivyo wenye tabia ya kujihusisha na rushwa waache mara moja,” alisema. Aliwataka makamishna na makamanda wote wa polisi nchini kuhakikisha wanasimama kidete kukomesha rushwa na kuwataka kila mmoja kwa nafasi yake kukemea vitendo hivyo. “Kuna askari polisi wanachukua rushwa hadharani wanaposimamisha mabasi na ninyi makamanda wa mikoa mpo,” alisema. Pia aliwataka makamishna na makamanda wa mikoa kuwaandaa askari vijana ambao watashika nafasi zao ili wao kurejea makao makuu kwa utungaji wa sheria na ushauri. “Ni vyema kuwa na damu changa itakayoweza kufanya kazi kwa nguvu zaidi kuliko kung’ang’ania nafasi hizo za ukamishna,” alisema. SARE ZA POLISI Pia IGP Sirro alitolea ufafanuzi kuhusu sare za jeshi hilo akisema kila sare ivaliwe sehemu yake husika na kwa tukio maalumu. “Utamkuta askari mkubwa amevaa sare za mapambano, amezivaa sehemu ambayo si husika kama vile kwenye mikutano ya vyombo vya habari au amevaa akiwa ofisini akifanya kazi za utendaji, vazi lile halitakiwi katika shughuli kama hizo,” alisema. IGP Sirro aliwashangaa pia baadhi ya askari kutojua kuimba wimbo wa maadili ya Jeshi la Polisi, na kusisitiza kila askari anatakiwa kujifunza kuuimba.
3
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza  hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi.  Kwa misingi kama hiyo sisi kama  chombo cha habari  tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk.  Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia.  Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”.  Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi,  Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii.  Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo.  Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge.  viongozi  wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo.
5
Uwezeshaji huo upo katika kuwapatia elimu ya ujasiriamali pamoja na kuwawezesha vitendea kazi vya kisasa ili waweze kufikia ndoto zao.Mikoa iliyofikiwa na Airtel kupitia mradi huo wa jamii ni pamoja na Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Kagera, Manyara na Dodoma.Mkuu wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano alisema mikoa 6 tayari imefaidika na shilingi milioni 125 za mradi wa Airtel Fursa na bado mradi unaendelea.Alisema Airtel kila wiki hutumia Sh milioni 20 kwa ajili ya makundi mawili au vijana wawili watakaojitokeza na kuomba kuwezeshwa na mradi wa Airtel Fursa, alisema Singano.“Awali mwaka huu tulitenga jumla ya Sh bilioni moja kwa ajili ya kuwasaidia vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 24 kuweza kutumia fursa walizonazo na kujiajiri wao wenyewe pamoja na wengine, sasa pesa hizi zipo na zinawasubiri,“alieleza Singano.Katika siku 90 wamesaidia vijana wanaojishughulisha na biashara au ujasiriamali katika utunzaji wa mazingira, ufugaji, kilimo cha kisasa pamoja na biashara mbalimbali, zikiwemo za saluni kwa wanawake, ufundi seremala, uvuvi, pamoja na bucha la nyama kwa familia.Mpango wa Airtel Fursa unawalenga vijana walio katika umri wa miaka 18 hadi 24. Ili kijana ashiriki au kufaidika na Airtel Fursa atatakiwa kutuma ujumbe mfupi kwenda kwa namba 15626 au barua pepe kwa airtelfursa@tz.airtel.com.
5
SHILINGI bilioni 107.8 zitakazolipwa na washitakiwa 467 wa kesi za uhujumu uchumi nchini, zitatumika katika mambo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa hospitali, barabara, kulipa mishahara na mengineyo mengi. Kurejeshwa kwa fedha hizo, kunatokana na ushauri wa Rais John Magufuli alioutoa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Biswalo Mganga kuona kama sheria inaruhusu kwa watuhumiwa wa kesi za uhujumu uchumi kukiri makosa yao, kuomba msamaha na kuwa tayari kurejesha fedha na mali za serikali. Rais Magufuli alitoa ushauri huo Septemba 22, mwaka huu Ikulu jijini Dar es Salaam, alipokuwa akiwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua. Alitoa siku saba kwa DPP kukamilisha kazi hiyo. Jana, DPP Mganga alitoa taarifa kwa Rais Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kukamilisha kazi hiyo. Katika taarifa yake, Mganga alimweleza Rais kuwa washitakiwa 467 wanaokabiliwa na kesi za uhujumu uchumi, walikubali kuandika barua za kukiri kosa, kuomba msamaha na kukubali kurejesha fedha jumla ya Sh bilioni 107.8. Kufanikiwa kwa jambo hilo, kunatokana na kuwepo kwa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20, inayohusu mashauriano ya kukiri kosa, ambayo Rais aliisaini Septemba 19, 2019. Ikiwa serikali itaamua kuzitumia fedha hizo, kujenga barabara za lami, inaweza kujenga jumla ya kilometa 107 za barabara za lami kwa wastani wa Sh bilioni 1 kwa kila kilometa. Lakini, pia kama itaamua kujenga vituo vya afya kwa gharama ya Sh milioni 400 kwa kila kituo, itaweza kujenga vituo vya afya 268. Kiasi hicho cha fedha, pia kinaweza kutumika kulipia elimu bure kwa wanafunzi kwa miezi minne kwa wastani wa Sh bilioni 23 kila mwezi pamoja au kujenga daraja moja la juu kama la Mfugale lililopo Tazara Dar es Salaam ambalo liligharimu Sh bilioni 100. Kwa mujibu wa DPP, miongoni mwa washitakiwa hao 467, kuna ambao wako tayari kulipa jumla ya Sh bilioni 7.88 wakati wowote kuanzia jana. Wengine wako tayari kulipa jumla ya Sh bilioni 5.7.Alifafanua kuwa katika kundi hilo la watu 467, kuna ambao wako tayari kulipa moja kwa moja jumla ya Sh bilioni 13.6, lakini kundi jingine wako tayari kulipa kwa awamu jumla ya Sh bilioni 94.2, hivyo kufanya jumla ya Sh bilioni 107.8. “Kwa hiyo Mheshimiwa Rais, jumla ya washitakiwa wa kesi za uhujumu uchumi 467 wako tayari kurudisha jumla ya Sh bilioni 107.8, lakini pia Ijumaa iliyopita kuna mtu mmoja aliitikia wito huu na kukiri kosa lake mahakamani na kulipa Sh bilioni 1.4 na faini ya Sh milioni 5,” alieleza DPP. Aliongeza, “Ijumaa hiyo hiyo, kuna mtu alikuwa na gramu 2,123.64 za madini vito yenye thamani ya Dola 15,876.66 sawa na Sh milioni 36.5, naye alikiri makosa yake na kulipa na madini hayo yalitaifishwa, pia wapo watu ambao wamekubali kurudisha mali zikiwemo gramu 33.2 za dhahabu, kilo 18 za Tanzanite na kilo 35 za madini vito.”Kwa kuwa jambo hilo lipo kisheria, DPP alimweleza Rais kuwa ofisi yake inalazimika kufanya uchambuzi mzuri na wa kina ili kuona ni mambo yapi wanaweza kukubaliana na yapi hawatakubaliana nayo, kurekebisha aina ya mashitaka na kwenda nayo mahakamani ili washitakiwa hao walipe mahahamani. Alisema utaratibu huo utazuia mwanya wowote wa mtu kuibuka hapo baadaye na kuishitaki serikali. Ili ofisi yake ipate muda wa kutosha wa kukamilisha kazi hiyo, Mganga alimwomba Rais amwongezee siku tatu kutokana na changamoto alizokumbana nazo ikiwemo barua kuandikwa kwa mkono, baadhi ya washitakiwa walioko magerezani kukosa nafasi ya kuandika barua mapema na wengine walikuwa wakihudhuria kesi zao mahakamani hivyo hawakupata nafasi ya kuandika barua hizo. Magufuli ashangaa Pamoja na kukubali ombi la DPP na kumwongezea siku saba, Rais Magufuli alishangaa kuona mwitikio mkubwa wa washitakiwa kuandika barua za kukiri makosa, kuomba msamaha na kukubali kurejesha fedha. Rais Magufuli alisema watu 467 ni wengi, licha ya kuwepo kwa baadhi yao kushindwa kuandika barua kutokana na sababu mbalimbali. Alimpongeza DPP na watendaji wake, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Polisi na Mahakama kwa kazi kubwa wanayoifanya.“Nakupongeza DPP na watendaji wako, ofisi yako inafanya kazi nzuri na tumekuwa tukishuhudia ukipata ushindi katika mashauri mbalimbali yanayoihusu serikali, pia tunashuhudia madini kutaifishwa: sikutegemea wangejitokeza watu 467, natumaini hawatarudia makosa yao, kama wapo waliokwamishwa au kukwama kuandika barua, basi mimi nakuongezea siku saba zingine,” alisema Rais Magufuli. Aliongeza, “Fedha hizi zitatusaidia katika kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa hospitali, barabara, kulipa mishahara na mengine mengi.” Kwa mujibu wa Rais, baada ya muda wa nyongeza wa siku saba kwisha, watakaoshikwa kwa makosa ya uhujumu, sheria ichukue mkondo wake. Alisisitiza kuwa siku saba alizoziongeza, zinawahusu wale tu ambao walikwama kuwasilisha barua zao kwa wakati au barua zao kukwama magerezani na kwenye ofisi za DPP mikoani. Alitahadharisha kuwa msamaha unaotolewa na serikali ni hakika na siyo mzaha, kama baadhi ya watu wanavyopotosha. Alisema serikali haiwezi kutoa msamaha wa majaribio kwa kumtega mtu. Aliongeza kuwa baadhi ya washitakiwa, wanadanganywa na mawakili wao ili waendelee kuwachomoa fedha. “Wenye nia ya kutubu na kurudisha fedha wasiwe na wasiwasi, kukiri kwenu hakutatumika kama ushahidi kama baadhi ya watu wanayopotosha, siwezi kufanya kazi ya kitoto namna hii,” alisisitiza Rais Magufuli. Ataka waanze kuachiwa Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alimtaka DPP kuharakisha mchakato huo ili watu hao waanze kutoka na kwenda kuungana na familia zao pamoja na kuendelea na shughuli zao za kimaisha. Alivitaka vyombo vya upelelezi, Magereza na Ofisi ya DPP kushirikiana katika hilo. Alisema mwenye mamlaka ya kufuta kesi ni Ofisi ya DPP pamoja na Mahakama. Alisisitiza kwa kuwa watu hao waliingia kwa njia ya mahakama, basi watoke kwa njia ya mahakama. Alisema kama watu hao wataendelea kukaa ndani kwa muda mrefu, maana ya msamaha huo inaweza isiwepo na kusisitiza kuwa asiwepo mtu wa kulazimishwa kuomba msamaha.
3
FURAHA ya binadamu aliyekamilika hapa duniani ni kupata mtoto, hasa kwa wale ambao wamekubaliana kuishi pamoja (wanandoa). Hata hivyo, siku hizi watu wengi wanakabiliwa na matatizo ya uzazi. Tunashuhudia baadhi ya ndoa zikivunjika kutokana na wanandoa kushindwa kupata watoto, ni jambo linalohuzunisha. Mara nyingi wanawake ndio hutupiwa lawama inapotokea changamoto hiyo, lakini wataalamu wa afya wanaeleza kwamba hata wanawaume wanaweza kushindwa kuzalisha. Zipo pia simulizi za ndugu, jamaa na marafiki ambao hulazimika kwenda nje ya nchi kufuata matibabu ya kibingwa ili kupandikiza ujauzito. Uongozi wa Hospitali ya Kairuki (KH), Shule ya Uuguzi Kairuki (KSN), Hospitali ya Kairuki (KH) na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki  (KHMU) unakusudia kuanzisha huduma ya kupandikiza ujauzito nchini, ikiwa ni sehemu ya kumbukizi ya Hubert Kairuki aliyefariki mwaka 1999. Mwasisi huyo alifariki dunia wakati miradi yake hiyo ikiwa michanga na sasa imekuwa kimbilio la wananchi wengi. Daktari Bingwa wa Wanawake hospitalini hapo, Clementina Kairuki anasema kwa kawaida iwapo mke na mume wanahitaji kupata mtoto wanapaswa kushiriki tendo la ndoa mara mbili hadi tatu kwa wiki. “Ikiwa watashiriki kwa kipindi cha mwaka mmoja huku wakiwa hawatumii kinga yoyote lakini wakashindwa kupata mtoto hapo tunaanza kufanya uchunguzi wa awali kwanini hali hiyo ipo. “Hapo tunaanza kuhesabu kwamba kuna tatizo hivyo tunamfanyia uchunguzi, kwa sababu katika kipindi cha mwaka mmoja wanakuwa na uwezekano wa kupata mimba kwa kiwango cha asilimia 86. “Kipindi cha mwaka wa kwanza huwa ni cha kusubiri, lakini ikiwa watakaa zaidi hadi mwaka wa pili hapo inabidi tuwafanyie uchunguzi wa kina, lakini kabla ya yote tunaangalia ushiriki wao katika tendo,” anasema.  Ukubwa wa tatizo Anasema Shirika la Afya Duniani (WHO) linabainisha kuwa watu milioni 48 duniani wanakabiliwa na tatizo la kutopata ujauzito. “Lakini matokeo hayo yalikuwa ni ya uchunguzi wa watu ambao walikaa kwa kipindi cha miaka mitano bila kupata ujauzito, tafsiri ni kwamba inabidi wawe wamekaa miaka miwili bila kupata ujauzito hivyo, WHO mwaka 2014 likasema kwa waliokaa miaka miwili hadi miwili na nusu maana yake watu milioni 12 ndiyo wenye tatizo la kutopata ujauzito,” anasema. Anasema kutokana na matokeo ya utafiti huo, WHO ilitangaza tatizo hilo kuwa ni janga. “Hapa nyumbani (Tanzania) tuna matokeo ya utafiti ambao ulifanyika zamani kidogo, unaonesha asilimia 20 ya mtu mke na mume walio katika umri wa kupata ujauzito wanakabiliwa na changamoto hiyo,” anasema. Anasema katika kliniki yao, asilimia 30 ya wanawake na wanaume wanaowahudumia wanakabiliwa na tatizo hilo na kwamba kati yao asilimia mbili hadi 10 wanashindwa kabisa kutatuliwa matatizo yao na hivyo kuhitaji njia mbadala (kupandikiza). Anasema changamoto wanayoiona ni kwamba mara nyingi wanawake ndiyo ambao hujitokeza na kugundulika mapema huku wanaume wakija baadae kuhudhuria kliniki.  Visababishi “Wote wanapaswa kuchunguzwa, mwanamume anaweza kuchangia tatizo hili kwa asilimia 40 hadi 50 na wanawake hivyo hivyo. Ni kwa asilimia tano tu wanaweza kuchangia wote wawili kushindwa kusababisha ujauzito,” anasema. Dk. Kairuki anasema tafiti zinaonesha wanawake wengi nchini hushindwa kupata ujauzito kutokana na kuziba kwa mirija ya uzazi kuliko wakina baba. Anataja sababu za kuziba kwa mirija kuwa ni pamoja na kutoa mimba ovyo, kujifungua katika mazingira ambayo si salama ambako kunaweza kusababisha maambukizi na hatimaye kuziba mirija ya uzazi. Anasema iwapo mwanamke atatoa mimba na asisafishwe vizuri, matokeo yake ni kupata maambukizi yanayoweza kusababisha mirija ya uzazi kuziba. Pia mjamzito anapochelewa kujifungua na kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kutoa mtoto kunaweza kusababisha maambukizi. Dk. Clementina anasema wapo wengine ambao wamezaliwa na matatizo ya homoni, kwamba zinakuwa hazijawiana inavyotakiwa na hivyo kushindwa kupata ujauzito. “Mtu anaweza pia kuwa amezaliwa huku viungo vyake vya uzazi vikiwa havijakamilika, kupata maradhi mbalimbali ikiwamo saratani au uvimbe kwenye kizazi kunaweza kumfanya mwanamke asibebe ujauzito. “Kuna asilimia 15 ya wanandoa ambao hawapati ujauzito na sababu hazijulikani, yaani ukiwachunguza unakuta hawana tatizo lolote na wanashiriki vema kabisa tendo,” anasema.  Wanaume nao wana matatizo Dk. Kairuki anasema kwa upande wa wanaume huwa wanaangalia vitu vinne ikiwamo ubora wa mbegu zake. “Ule wingi wa mbegu anaotakiwa kutoa mara moja kiwango cha chini kinapaswa kuwa milioni 39 kwa mkupuo wa kwanza, ile kasi yake inapaswa kuwa angalau asilimia 32 na ‘concentration’ katika ujazo huo iwe mililita moja,” anabainisha. Anasema huwa wanaangalia pia umbo la mbegu zake jinsi zilivyokaa, ambapo wakichunguza huwa wanajua iwapo zipo sawa sawa kama zinavyopaswa au la. Anasema kuna akina baba hawana mbegu kabisa au zipo chache na hazikidhi kiwango kinachotakiwa. “Hii inatokana na mambo mengi, inawezekana ikawa ‘chromosome’ zake hazipo sawa sawa au anakuwa anatengeneza mbegu chache mno. Kuna vitu vingi vinasababisha matatizo ya genetics, homoni hazitoshi au viungo vyake havijakamilika,” anabainisha. Anasema kama mtu anakabiliwa na ugonjwa wa kisukari huweza kumsababishia kushindwa kufanya vema tendo la ndoa au kupungukiwa nguvu hivyo kushindwa kutoa mbegu au akatoa kwa kiwango cha chini. “Wengine wanashindwa kabisa kutoa yale majimaji kwa sababu mbegu hutoka zikiwa na majimaji yake, hali ya hewa nayo inaweza kusababisha tatizo hasa katika joto jingi, au kutokunywa maji ya kutosha pia ni kisababishi,” anasema.  Matibabu Anasema pale wanapogundua tatizo kuna njia nyingi huzitumika kuwatibu wahusika ikiwamo za vidonge na upasuaji. “Tunaweza kuwatibu kwa kuwapatia dawa maalumu za vidonge wote wawili au tunafanya upasuaji wa kuzibua mirija kama imeziba. Kama mayai ya mama hayakomai vizuri tunaweza kufanya upasuaji katika vifuko vya mayai yake na yakatoka yakiwa yamekomaa vizuri,” anasema. Anasema wanaweza kufanya upasuaji huo kwa njia ya kisasa ya ‘laparascopic’ na mama akaeendelea na shughuli zake kama kawaida baada ya muda mfupi. “Ikiwa njia hizo zitashindikana, basi hutulazimu kupandikiza. Tunaweza kuchukua mbegu za baba na kuzitayarisha maabara huku tukisubiri mayai ya mama yakomae, tunachukua zile mbegu za baba na kuweka kwa mama kupitia njia ya uke. “Njia hii imeanza kutumika tangu miaka ya 1970 lakini ili kuitumia inapaswa mirija ya mama iwe wazi (haijaziba), kama imeziba inabidi kutumia njia nyingine ikiwamo ile ya IVF. “Mwaka 1978 alipatikana mtoto wa kwanza kwa kutumia njia hii ya IVF, baada ya hapo zikagundulika pia njia zingine ambazo zinaweza kutumika kwa wanandoa wenye shida ya uzazi,” anasema. Dk. Clementina anasema ipo njia nyingine ambapo mbegu za baba huhifadhiwa na mayai ya mama hutayarishwa kwa kuchomwa sindano maalumu. “Kwa kawaida mayai mawili hukomaa kwa pamoja, lakini kwa njia ya kitaalamu tunaweza kuvuna hata mayai 20 kwa mkupuo na kuyapeleka maabara,” anasema. Anaongeza: “Mwanamume anaweza kutoa mbegu kwa njia ya kawaida ya kujamiiana au kwa kupiga punyeto, huwa tunamshauri jinsi ya kufanya na muda gani akae ndio azitoe. “Ikishindikana tunampatia dawa maalumu ya kumchangamsha ili zitoke zenyewe na ikiwa hazitoki kabisa tunaweza kuzichukua kitaalamu kwa upasuaji kutoka kwenye korodani zake na kuzipeleka maabara.” Anasema wakizifikisha maabara huziweka pamoja na kwamba baada ya siku mbili hadi tano huwa tayari zimetengeneza kijusi ambacho huchukuliwa na kuingizwa katika tumbo la uzazi la mama kwa njia ya uke. “Baada ya hatua hiyo, mama anapewa muda wa kupumzika kwa dakika 15 kisha anakwenda zake nyumbani akiwa tayari ana ujauzito. “Mimba hiyo huwa haina tofauti na zile zilizotungwa kwa njia ya kujamiiana, licha ya kwamba hii huwa imetayarishwa maabara, kiumbe kinakua kikiwa maabara na tunakitumbukiza kwa njia ya uke kwenda kwenye tumbo la uzazi ambalo nalo linakuwa limeandaliwa kukipokea. “Kwa njia ya IVF tunakuwa tumechukua mayai ya mama na kuyamwagia mbegu za baba ambazo hufuata yale mayai, kasi yake huwa kubwa zaidi kuliko njia ya kawaida kwa sababu yanakuwa yameandaliwa. “Kwa njia ya IX tunachofanya ni kuchukua yai la mama na mbegu ya baba kisha tunachomeka moja kwa moja wakati njia ya IVF tunaingiza zile mbegu nyingi kwa pamoja,” anabainisha.  Njia mbadala Daktari huyo anasema wapo wanawake ambao hawana mayai au wanayo lakini hayakidhi viwango hasa wale walio na umri mkubwa kwa kuwa yanakuwa yamepoteza ubora, hivyo njia hii huwasaidia. “Nchi za wenzetu, wana benki ya kuhifadhia mayai na mbegu za uzazi, zinahifadhiwa katika chumba chenye nyuzi joto 196 ambayo ni baridi kali sana na kuna kemikali ambazo hutumika kuhifadhia, zinaweza kukaa hata miaka 50 ndani ya chumba hicho,” anasema. Wizara Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubisya anasema mpango huo ni mzuri na wa kupongeza kwa kuwa utasaidia wengi. “Nawaomba muendelee na mshikamano huo wa kubuni mambo yanayohusu tiba kwa maslahi ya wananchi, wazo hili litakapoanza litasaidia wananchi wengi. “Hivi sasa serikali ina mambo mengi ya kufanya, si vibaya watu binafsi wakiwa na miradi itakayokwenda sambamba na msaada kwa wananchi,” anasema.
0
Na ABRAHAM GWANDU-Arusha WASOMI, wadau wa elimu na wananchi wa kawaida wamekosoa tamko la Waziri  wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, wakisema kwamba halijafanyiwa utafiti na halitekelezeki kisheria. Mwishoni mwa wiki, akiwa kwenye mahafali ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Ndalichako alisema kuanzia mwakani mwanafunzi yeyote hatajiunga na masomo ya Shahada bila kupitia kidato cha sita. Alisema mfumo wa elimu huria umechangia kuzalisha wasomi butu kwa kupokea wanafunzi dhaifu kitaaluma. Wakizungumzia tamko hilo kwa nyakati tofauti katika maeneo mbalimbali nchini, baadhi ya wasomi  walisema kabla ya waziri kuanza kutoa amri na matamko, alitakiwa kufanya utafiti kujiridhisha juu ya agizo lake hilo. “Profesa Ndalichako hajasema ametoa wapi ujasiri wa tamko lake, ni kwa utafiti upi aliofanya yeye au hata kukasimu taasisi kwa niaba yake ili ifanye utafiti na kuja na majibu kuwa kidato cha sita ndicho kiwango bora cha kumpitisha mtu kusoma shahada ya kwanza? “Binafsi naona haya ni matamko ya kisiasa yasiyoweza kutekelezwa kisheria, arekebishe sheria kwanza ndio aje kutoa tamko la kurekebisha mfumo wa elimu, vinginevyo anaweza kuharibu kuliko waliomtangulia,” alisema mkuu wa chuo kikuu maarufu mkoani Arusha ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini. Naye Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Tawi la Makumira, Mchungaji Profesa Josef Parsalao, alisema pamoja na lengo zuri la kurekebisha mfumo wa elimu, badala ya kuanza na amri na matamko, Serikali ilitakiwa kurekebisha kasoro zilizopo hatua kwa hatua. “Sijui yeye Ndalichako alipitia hatua zipi za elimu, lakini upo ushahidi wa kuwapo kwa wasomi wengi wakiwamo wale wanaofundisha vyuo mbalimbali nchini, kupitia ngazi ya chini kabisa ya cheti na sasa ni maprofesa na walifundisha hawa wanaobeza ngazi hizo. “Wapo majaji ambao walianza kazi ya ukarani mahakamani, wakajiendeleza kwa kusoma Chuo cha Mahakama Lushoto ngazi ya cheti, sasa ni madaktari na maprofesa wa sheria tunawategemea,” alisema Profesa Parsalao. BANA Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, yeye alisema haamini kama alichosema Waziri Ndalichako ni tamko na uamuzi wa Serikali, kwani suala hilo haliko kwenye sera ya elimu na kuonya kuwa alifute haraka kwani hiyo si njia sahihi ya kuboresha elimu nchini. Dk. Bana alikwenda mbali zaidi kwa kutoa mfano wa jinsi yeye alivyosoma kupitia mfumo huo unaopingwa na Ndalichako hadi hapo alipofikia. “Kama kachukua uamuzi huo, nafikiri amekurupuka, kama anafikiria kidato cha sita ndiyo njia pekee, ameshauriwa vibaya na huo uamuzi aufute haraka sana na ni kinyume na utaratibu wa elimu kote duniani… utakuwa ni uamuzi wa dhambi ya asili na dhambi ya ubaguzi. Kama anataka njia ya kuboresha elimu aje tumfundishe. “Mimi binafsi sikupitia kidato cha sita na kuna maprofesa zaidi ya 20 au 40 ninaowafahamu, yupo Profesa Baregu (Mwesiga Baregu) hakusoma kidato cha sita, kuna Profesa Mathew Luhanga ambaye alikuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa miaka 14, yupo pia Profesa Cuthbert Kimambo ambaye alikuwa Mkuu wa Taaluma UDSM na wengine wengi, ni watu wanaoheshimika kote duniani,” alisema. PROFESA BAREGU Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT), Profesa Mwesiga Baregu, hakutofautiana na Dk. Bana. Yeye alisema mfumo uliopo unakubalika duniani kote na ndio ulioleta msemo wa ‘elimu haina mwisho’. “Kauli ya waziri imeonyesha umuhimu wa kuwa na tume ya kitaifa ya kushughulikia suala la elimu, kwa sababu kweli kuna tatizo la ubora wa elimu yetu na halipaswi kunyamaziwa, lakini hii si njia sahihi ya kulitatua. “Sijamwelewa waziri kwanini ameona diploma kwenda chuo kikuu ndiyo tatizo na kusema kuwa watu wote wana haki ya kujengewa mazingira ya kujiendeleza kielimu,” alisema Profesa Baregu. PROFESA MPANGALA Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ruaha mkoani Iringa (RUCO), Profesa Gaudence Mpangala, alisema anapinga uamuzi huo wa Profesa Ndachako kwani utawanyima watu uhuru wa kujiendeleza. Profesa Mpangala naye aliwataja baadhi ya maprofesa anaowafahamu ambao hawakupitia kidato cha sita na akasema wamekuwa msaada mkubwa kwa taifa. “Profesa Kimambo alikuwa mwalimu wangu wa Kiswahili, yeye alikuwa na elimu ya ualimu ‘Grade’ C wa shule ya msingi lakini amejiendeleza hadi amekuwa Profesa yupo pia Profesa Ndunguru na wengine wengi na waliopitia mfumo wa Cheti-Stashahada wanakuwa na uzoefu mkubwa kuliko wa kidato cha sita na wanafanya vizuri wakifika chuo kikuu,” alisema Profesa Mpangala. TAMONGSCO Akizungumzia kauli hiyo ya Profesa Ndalichako, Katibu Mkuu wa Vyuo na Shule Binafsi Tanzania, Benjamini Nkonya, alisema hawaelewi waziri huyo kutoa tangazo kama hilo ni kwa sababu watu wengi wamekuwa watumishi bora sana na wengi hawajasoma kidato cha sita au vinginevyo. “Wito wetu kwa Serikali ikamilishe mchakato kwa kupeleka rasimu ya sheria mpya ya elimu bungeni, ili pawepo na Baraza la Taifa la Elimu ambalo litakuwa na wawakilishi kutoka sekta ya umma, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na sekta binafsi kama TAMONGSCO, ambayo itaandaa nyaraka (regulations) zote kabla hazijawekewa sahihi na kamishna wa elimu,” alisema Nkonya. PROFESA MLAMA Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama, yeye alikubaliana na mawazo ya Waziri Ndalichako, akisema mfumo huo ni wa zamani na uliruhusiwa ili kutoa fursa kwa watu kusoma kwa kuwa nchi ilikuwa na wasomi wachache. “Sasa hivi kuna wanafunzi wengi wa kidato cha sita na fursa nyingi za kusoma kidato cha tano na sita zipo, tofauti na kipindi cha miaka ya nyuma, hakuna ulazima sana wa watu kutegemea njia yingine wakati wanaweza kusoma kidato cha sita na kuwa sawa na wengine darasani,” alisema. LALTAIKA Kaimu Mkuu wa Idara ya Ubunifu, Usimamizi wa Teknolojia na Ujasiriamali katika Taasisi ya Sayansi ya Nelson Mandela, Dk. Amani Laltaika, alipongeza hatua ya Profesa Ndalichako, huku akisema amegundua tatizo katika elimu na amethubutu kuchukua hatua ya kurekebisha kuliko waliomtangulia ambao hawakuchukua hatua yoyote. “Sifa ya kwanza ya kiongozi ni ubunifu na kutatua matatizo yaliyopo, nampongeza waziri kwa kugundua upungufu katika elimu yetu, kwa sababu walikuwapo mawaziri wengi katika nafasi aliyopo sasa, lakini hawakugundua,” alisema Dk. Laltaika. SIFA ZA TCU KUJIUNGA NA VYUO Mwezi Juni mwaka huu, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), ilitangaza utaratibu mpya kwa watahiniwa wa mwaka mpya wa masomo wa 2016 na 2017 wanaochukua shahada. Utaratibu huo mpya ulikuja baada ya miezi miwili tangu kutumbuliwa kwa watendaji wa tume hiyo kutokana na kudahili wanafunzi wasio na sifa na kusababisha kupewa mikopo na Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Pamoja na sifa hizo ambazo ziliwahusu waliomaliza kidato cha sita, pia sifa hizo zilieleza kuwa wale watakaodahiliwa kujiunga na vyuo ni pamoja na watakaokuwa na utambulisho wa sifa za kielimu za kidato cha nne kuanzia alama nne ambazo ni D na kupanda juu katika mchanganuo wa alama za ufaulu wa B+, ikiwa A=75-100, B+=65-74, B=50-64, C=40-49, D=35-39 na F=0-38. Sifa nyingine zinazotajwa ni wenye vyeti vya NVA daraja la tatu, wenye ufaulu si chini ya alama nne au sifa nyingine zinazokaribiana na hizo, ikiwa ni pamoja na zinazotambuliwa na Baraza ka Taifa la Mitihani (NECTA) na Elimu ya Mafunzo ya Ufundi (VETA). Watahiniwa hao watatakiwa kuwa na angalau GPA ya 3.5 kwa stashahada ‘NTA’ daraja la sita au wastani wa B kwa cheti cha ufundi ‘FTC’ katika mchanganuo wa alama A=5, B=4, C=3 na D=2 au wastani wa daraja la B+ kwa wenye stashahada za ualimu au wastani wa daraja B+ kwa kitengo cha afya kama tabibu wa magonjwa ya binadamu na nyingine au cheti na stashahada nyinginezo. Sifa nyingine zinazoangaliwa katika udahili huo ni pamoja na kuwa na ufaulu wa daraja la pili kwa wenye Stashahada zisizokuwa za NTA. Imeandaliwa na Abraham Gwandu (Arusha), Jonas Mushi na Mauli Muyenjwa (Dar)
3
Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa ziara ya Dangote ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho kikubwa cha Saruji Afrika Mashariki, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Abrahaman Shah alimweleza bilionea huyo namba moja Afrika kuwa, wakazi wa kijiji chake wameridhia kumpatia eneo kwa ajili ya ujenzi wa bandari na kwamba ni imani yao mradi huo utatekelezwa haraka iwezekanavyo.“Sisi wakazi wa Mgao tumekupatia eneo la hekari 2,500 la nchi kavu na bahari ili ujenge bandari, pia tunawapatia ukazi wa kudumu katika kijiji chetu, wewe, balozi na balozi mdogo wa Nigeria hapa nchini, wote ninyi kuanzia sasa ni wakazi wa kijiji cha Mgao,” alisema Mwenyekiti huyo na kuongeza; “Kijiji chetu kina wakazi 2026, Alhaji Dangote atakuwa mkazi wa 2029, Balozi Isihaka Majabu atakuwa mkazi wa 2027 na balozi mdogo Salisu Umaru atakuwa mkazi wa 2028…hawa ni wakazi wenzetu wa kijiji cha Mgao,” alisema.Aliongeza kuwa, wanamuomba mbunge wao, Hawa Ghasia kusimamia taratibu zingine za kiserikali kufanikisha lengo lao la kupatikana kwa bandari katika kijiji chao.“Suala hili limeridhiwa na wanakijiji wote, tunamuomba mbunge wetu asimamie kuhakikisha kazi hii inakamilika haraka iwezekanavyo ili wananchi wa Mgao na maeneo mengine wapate kukuza uchumi wao kupitia bandari hii ... wapo watakaoajiriwa na wengine watafaidika kutokana na ongezeko la mahitaji ya chakula na vitu vingine,” alisisitiza mwenyekiti huyo.Naye Alhaji Dangote aliwashukuru wanakijiji hao kwa kumpatia ardhi kwa ajili ya ujenzi wa bandari na makazi ya kudumu katika kijiji chao na kuwaahidi kuwa miezi sita tangu taratibu zingine za kisheria kukamilika na kukabidhiwa eneo hilo, ujenzi wa bandari utakuwa umekamilika.Balozi mdogo wa Nigeria nchini Salisu Umaru alitembelea eneo hilo na kuzungumza na wanakijiji hao ambapo walimthibitishia kuwa maelezo ya mwenyekiti wao ni sahihi na kwamba wanachoomba ulipaji wa fidia kwa baadhi ya maeneo uzingatie haki ili kuepusha migogoro.
5
Katika mchezo bao la kwanza lilisababishwa na makosa ya Kessy aliyekuwa akijaribu kumrudishia mpira kipa wake, Vincent Angban lakini ukawahiwa na Donald Ngoma na kufunga.Baadhi ya mashabiki wamekuwa wakilalamika kuwa huenda Kessy aliuza mechi ndio maana alifanya uzembe wa makusudi, jambo ambalo Mayanja alisema kama ni makosa yalitendeka kwa wachezaji wote.Akizungumza jana Dar es Salaam Mayanja alisema walijiandaa vizuri dhidi ya Yanga lakini kilichoshangaza wachezaji wake walicheza tofauti na kile walichoelekezwa.“Hatuwezi kusema ni Kessy peke yake, wachezaji wote hawakucheza kama nilivyowaelekeza sijui ni nini kilitokea,”alisema na kuongeza kuwa watu wamekuwa wakilalamika bila kujua matatizo ya kiufundi.Mayanja aliwashukuru mashabiki wa Simba kwa kuwaunga mkono katika mchezo huo huku pia akiwataka kutokata tamaa kwani kuna michezo mingine ya ligi inakuja.Alisema kwa sasa anaangalia mbele michezo ijayo katika kuhakikisha inafanya vizuri kama ilivyotokea kwa michezo mingine.Wakati Mayanja akiongea hayo, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga Jerry Muro alimpongeza Kocha huyo kwa kuwa muungwana.Alisema Mayanja alionyesha uungwana kwa kuwa aliona kuwa wachezaji wake waliteleza na sio kumlaumu mwamuzi au mchezaji.
4
ARODIA PETER NA MAULI MUYENJWA -DAR ES SALAAM ALIYEKUWA Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, ameufananisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuwa ni kama ‘ndoa ya jinsia moja’, kwa kuwa pande zote mbili zina haki sawa, hata kama ukweli utapindishwa. Akitoa mada ya maslahi ya Zanzibar katika Katiba mpya wakati wa Mkutano Mkuu wa Kikatiba Dar es Salaam jana, Othman alisema kukwama kupatikana kwa Katiba mpya Tanzania ni hofu ya kuvunjika kwa Muungano, baada ya walio wengi kupendekeza mfumo wa Serikali tatu. Pia aliponda hisia hizo kwa kusema zinajengwa kinadharia ili kuwatia hofu wananchi. Othman, aliyejiuzulu wadhifa huo wakati wa Bunge Maalumu la Katiba la mwaka 2014, alisema ndoa za jinsia moja ni falsafa tu, lakini haziwezi kubadili ukweli wa maumbile halisi ya wahusika.  “Ukweli ndoa ya jinsia moja ni kwa falsafa tu, haibadilishi ukweli kuwa yule mwanamume anayejifanya mwanamke atabaki kuwa mwanamume, hata yule mwanamke atabakia mwanamke tu na ipo siku mmoja akiudhiwa anaweza kumwambia mwenzake hata mimi mwanamke, mwanamume kama wewe usinifuatilie,” alisema Othuman. Katika mada yake hiyo, Othman alizungumzia kwa undani historia ya kero za Muungano tangu utawala wa marehemu Aboud Jumbe na alisema kilio chake juu ya kero hizo kiligharimu wadhifa wake.   Pia alisema ingawa mambo ya Muungano kwa idadi ni 22 kama yalivyoainishwa na Katiba ya mwaka 1977, lakini ukweli ni kwamba mambo ya Muungano hayajulikani ni mangapi. “Dalili ya kwanza inayoonesha kwamba baadhi ya mambo yanafanywa kuwa ya Muungano lakini si kweli, ikiwamo masuala ya bima yanayosimamiwa na Kamishna wa Bima. “Lakini pia Bunge limekuwa likitunga sheria na kuzifanya za Muungano, hata kwa mambo ambayo hayamo katika orodha ya Muungano, kwa mfano sheria ya proceeds Crimes Act ya 1991,” alisema. Pia alisema Serikali tatu hazina tatizo lolote na hofu inayojengwa si halisi, bali ni ya kupandikizwa kwa sababu si kweli kwamba Serikali tatu zitavunja Muungano. Othman alisisitiza kuwa, Muungano uliopo wa Serikali mbili ni kama mmoja ameamua kukubaliana na hali hiyo ili mambo yaende, lakini ukweli hata Zanzibar yenyewe ilihitaji kuwa na mamlaka yake huru. Wakati huo huo, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. James Jesse, alisema ili mchakato wa Katiba mpya uweze kuendelea, ni lazima iundwe sheria ya amri ya rais na kupelekwa bungeni kuruhusu mchakato huo. Alisema vifungu vipya vya sheria vinatakiwa kutengenezwa ambavyo vitatoa mwongozo mpya wa nini cha kufanya, kwa kuwa vile vya awali vimepitwa na wakati na haviwezi kutekelezeka.
3
MBUNGE wa Jimbo la Manonga lililopo Igunga mkoani Tabora Seif Gulamali amempongeza Rais John Magufuli kwa kuteuliwa wa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya maendeleo ya nchi zilizopo Kusini mwa Bara la Afrika (SADC) pamoja na kufanikisha vyema mkutano wa SADC uliomalizika Jumapili Jijini Dar es Salaam.Akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari Gulamali pamoja na mambo mengine pia alimpongeza Rais Magufuli na watanzania wote kutokana na lugha ya Kiswahili kuchaguliwa kuwa moja ya lugha itakayotumiwa katika mikutano ya SADC, suala alilosema litazidi kulitangaza taifa la Tanzania.Alisema kitendo cha Rais Magufuli kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC katika mkutano huo huo kunazidi kuiletea heshima Tanzania ambayo tangu ilipoapata uhuru wake Mwaka 1961 imeendelea kuwa kitovu kikuu cha Amani miongoni mwa Mataifa mbalimbali katika Bara la Afrika na Dunia kwa ujumla.Aidha alisema pamoja na kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC pia mkutano huo wa wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo ulifana chini ya Uenyeji wake huku hotuba yake ikigusia maeneo muhimu kwa ajili ya Maendeleo ya Jumuiya hiyo na Wananchi wake, jambo alilodai kuwa litazidi kuhimarisha Umoja na mshikamano wa Nchi hizo kama alivyokuwa ameligusia katika hotuba yake alipokuwa akifunga mkutano huo.Alisema kauli ya Rais Magufuli kusema kuwa Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano unaohitajika kwa wanachama wa SADC ili kuharakisha jitihada za kuleta maendeleo fungamani, linaonyesha ni kwa namna gani Kiongozi huyo ana kiu ya kuziona nchi zote zilizomo ndani ya SADC zinapiga hatua zaidi za kimaendeleo kama alivyo na kiu hiyo kwa Tanzania .“Pamoja na kuzitaka nchi Wanachama kutoa kipaumbele katika suala zima la Usalama, Amani na Utulivu pia alizitaka kuboresha eneo la ukuaji wa Viwanda, Biashara na utengenezaji wa fursa za kibiashara, jambo ambalo ni muhimu katika uzalishaji wa Ajira na Maendeleo yake na Wananchi kwa ujumla, anastahili pongezi kwa kuliona hili”alisema Gulamali.Alisema kimsingi mambo mengi ambayo Rais Magufuli amegusia katika hotuba yake hiyo yana akisi yale anayoendelea kuyafanya hapa nchini ambayo kwa kiasi kikubwa matokeo yake yanaonekana kwa kadri siku zinavyozidi kwenda huku akitoa rai kwa Mataifa Wanachama wa SADC kuyatekeleza ili malengo yaliyokusudiwa yaweze kufikiwa.Gulamali alisema hatua ya Rais Magufuli kuzitaka nchi wanachama wa Jumuiya hiyo kuweka mkazo katika usimamizi wa rasimali zake una maana kubwa katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi miongoni mwa nchi wanachama ambapo pato lake la ukuaji wa uchumi kwa Taifa ni wastani wa asilimia 22 katika kipindi cha Mwaka 2018.Aidha kuhusu lugha ya Kiswahili kuchaguliwa kuwa miongoni lugha ya nne za kimataifa kutumika katika mikutano ya SADC, ni fahari kwa Tanzania kwa kuwa itazidi kulitangaza Taifa na kuzidi kuliletea heshima katika Mataifa mbalimbali huku tayari lugha hiyo ikitajwa kuzungumzwa katika mataifa 10 Duniani.Aliwataka watanzania kutumia fursa hiyo adhimu ya kutumika kwa lugha hiyo kwenda kutafuta fursa mbalimbali katika Mataifa hayo ili kuzidi kukitangaza pamoja na kujiingizia kipato kutokana na Ajira zitakazoendelea kutolewa ndani ya nchi hizo.
3
DARFUR, SUDAN KIKOSI maalumu cha kijeshi nchini Sudan kimewashambulia raia katika eneo la Kusini mwa jimbo la Darfur.  Watu saba wameuawa na wengine zaidi ya ishirini wamejeruhiwa.  Taarifa hii imetolewa na wanaharakati katika eneo hilo pamoja na kundi moja la waasi katika eneo hilo linalokumbwa na machafuko. Mashambulizi hayo yametokea wiki moja baada ya kundi la kujihami linalohusishwa na serikali kuvamia kambi moja Kaskazini mwa Darfur na kuwauwa watu 13. Msemaji wa kundi la waasi linalojiita vuguvugu la ukombozi wa Sudan Abdel-Rahman al-Nayer, amesema shambulizi la hivi punde zaidi lilifanywa siku ya Alhamisi na watu waliokuwa wamejihami waliowafyatulia risasi watu waliokuwa wakielekea katika mashamba yao katika mji wa Gereida umbali wa kilomita 107 Kusini mwa Darfur. Ghasia katika jimbo la Darfur zinahatarisha uthabiti wa kisiasa katika serikali ya mpito.  Mnamo mwezi Aprili mwaka jana, vuguvugu linalotaka demokrasia lilimuondoa madarakani kiongozi wa muda mrefu Omar al-Bashir na kuanzishwa serikali ya mpito inayowajumuisha viongozi wa kijeshi na kiraia.
2
ALIYEKUWA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amemshukuru Rais John Magufuli kwa msamaha aliomtangazia kutokana na sauti yake ya kumsema kuvuja mtandaoni.Jana, Rais Magufuli alitangaza hadharani kuwa amewasamehe January na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM) baada ya sauti zao za kumsema vibaya kuvuja kwenye mitandao ya kijamii.Alitangaza msamaha huo jana jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa Bodi ya Wahandisi, Wakandarasi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi na wadau wengine wa sekta ya ujenzi.January alipoulizwa na gazeti hili kuhusu msamaha huo wa Rais Magufuli, alijibu kwa ujumbe mfupi wa maneno katika simu ya mkononi (sms) kuwa, “Namshukuru Rais.”Uteuzi wa mwanasiasa huyo kijana ulitenguliwa na Rais Magufuli Julai 21, mwaka huu, huku nafasi yake ikichukuliwa na George Simbachawene aliyewahi kuwa Waziri wa Tamisemi katika utawala wa Rais Magufuli.Lakini jana Rais Magufuli alisema hivi karibuni kuna baadhi ya watu walimtukana kupitia mitandao ya kijamii na baada ya kuzisikiliza sauti zao kwa makini, ajiridhisha na kuthibitisha kuwa sauti hizo ni zao kwa asilimia 100.Aliwataja baadhi ya watu hao kuwa ni January Makamba na Ngeleja ambao baada ya kufanya kosa hilo na sauti zao kuvuja, waliamua kwenda kumuomba msamaha.“Nikafikiria na kisha nikasema, nikiwapeleka kwenye Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) adhabu yao ingekuwa kubwa sana, wawili ambao ni Makamba na Ngeleja walikuja kuniomba msamaha, nami nikawasamehe ili nisibaki na maumivu moyoni,”alieleza Rais Magufuli.Alisema kwa kuwa binadamu wote ni watoto wa Mungu, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kujenga tabia ya kusamehe ili kuishi kwa upendo.January ni nani? Ni mbunge wa Bumbuli mkoani Tanga.Alizaliwa mwaka 1974 mkoani Singida. Alihitimu Shahada ya kwanza ya masomo ya amani (Peace Studies) katika Chuo cha Mtakatifu Yohana kilichopo Minnesota nchini Marekani.Alihitimu Shahada ya Pili ya Sayansi kuhusu Uchambuzi na Usuluhishi wa Migogoro katika Chuo Kikuu cha George Mason nchini Uingereza.Amewahi kufanya kazi ya Ofisa wa Daraja la Pili wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na pia aliwahi kuwa Msaidizi wa Rais.Pia aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.Katika serikali ya sasa alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) hadi mwezi Julai mwaka huu.Ngeleja ni nani?Ni mbunge wa Sengerema mkoani Mwanza.Alizaliwa mwaka 1967 na alisoma shule za sekondari Mpwapwa mkoani Dodoma na Ihungo mkoani Kagera.Alihitimu Shahada ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1991; na Shahada ya pili katika Sheria alihitimu pia kutoka chuo kikuu hicho mwaka 1999.Aliwahi kuajiriwa katika Kampuni ya Uwakili ya PriceWaterHouse Coopers mwaka 1995-2000.Alikuwa Mwanasheria katika Kampuni ya Vodacom kutoka mwaka 2000 hadi 2005 alipogombea ubunge na kushinda.Aliwahi kuwa Naibu Waziri na pia Waziri wa Nishati na Madini katika Serikali ya Awamu ya Nne.
3
Aidha,wanatarajia kuboresha bandari ndogo za kwenye maziwa kuongeza ufanisi wa kutoa mizigo ikiwemo kuongeza ufanisi wa Usafiri wa Reli ambao kwa sasa unatoa bandarini asilimia 1.2 ya mizigo tu.Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Awadhi Massawe alimweleza hayo Waziri Mkuu wa Finland, Jyrki Katainen alipotembelea bandari hiyo, ikiwa sehemu ya ziara yake ya siku mbili nchini iliyomalizika jana.Massawe alikuwa akielezea mafanikio na changamoto zinazoikabili bandari hiyo na kubainisha kuwa ifikapo mwaka 2028 wanatarajia kupakua tani milioni 41.5 za mizigo.Akizungumza bandarini hapo, Katainen alisema amefurahishwa na uamuzi wa Serikali kuipa kipaumbele uboreshaji wa bandari kupitia mpango wa BRN kwani ikiwa na uwezo wa kutoa stahili pia biashara nchini itakuwa imara.Wakati huo huo, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyere aliwahakikishia watumiaji wa Bandari ya Dar es Salaam kuwa ni salama katika usafirishaji, uhifadhi na udhibiti wa kemikali mbalimbali hasa zile za salfa.Alisema tangu mwaka 2003 kumekuwa na sheria ya kudhibiti usafirishaji na uhifadhi wa kemikali nchi nzima. Katika bandari hiyo alisema upo uangalizi maalumu.
5
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Loata Ole Sanare amesikitishwa kuona baadhi ya wabunge wa mkoa huo kushindwa kushiriki vikao mbalimbali na shughuli za kiserikali bila ya kutoa taarifa jambo ambalo linawanyima wananchi fursa ya maendeleo.Sanare hayo kwa nyakati tofauti katika kikao cha Bodi ya Barabara pamoja na cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) vilivyofanyika jana katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Morogoro (Kigurunyembe) kilichopo mjini Morogoro. Kwa mujibu wa Sanare mkoa huo una jumla ya wabunge 14 kati yao 11 ni wa kuchaguliwa , lakini baadhi wameshindwa kuhudhuria vikao hivyo ili kutoa michango yao muhimu ya kuboresha bajeti jambo ambalo linawanyima wananchi fursa ya maendeleo.“Tupo hapa kujadili maendeleo ya mkoa wa Morogoro kwa ajili ya wananchi wetu , hivi ikitokea katika bajeti ijayo wakakosa fedha za miradi ya maendeleo nani wa kulamiwa,” alisema na kuongeza kuwa uwepo wao katika vikao kama hivi ungesaidia kutoa ushauri wa kuboresha mapendekezo yanayowasilishwa na watalaamu ili kusaidia miradi iliyopo maeneo yao kupata fedha.Sanare alisema kikao cha RCC kinashirikisha wajumbe wengi wakiwemo wanasiasa,lakini jambo la kushangaza mkoa una idadi ya wabunge 14 lakini walioudhuria katika vikao hivyo viwili ni wanne tu na kwamba wengine 10 hawakuonekana na bila kutoa taarifa ya udhuru wao wakiwemo wa kutoka chama tawala.“Mwenyekiti wa CCM mkoa na Katibu wako wa mkoa mpo hapa kwenye kikao hiki cha RCC, lakini wabunge wako hawapo hapa tena bila ya kutoa taarifa yoyote ile,” alisema Mkuu wa mkoa.Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Emmanuel Kalobelo alisema kuwa vikao hivyo vya Bodi ya Barabara mkoa na RCC vilisogezwa mbele ili kutoa fursa kwa wabunge hao kushiriki vikao hivyo baada ya kumalizika kwa vikao vya bunge na hiyo ni kutokana na umuhimu wao kwa ajili ya maendeleo ya mkoa huo.
3
Ashanti ndio inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 15 huku Polisi ikishika mkia kwenye nafasi ya nane ikiwa na pointi tatu. Aidha katika mechi za kundi B Polisi Morogoro itakuwa mwenyeji wa Kurugenzi FC ya Mafinga kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro, huku timu nyingine ya kundi hilo Kimondo FC ikicheza na Burkinafaso ya Morogoro kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.Kundi hilo linaongozwa na Ruvu Shooting yenye pointi 19 huku Burkinafaso ikishika mkia nafasi ya nane na pointi tatu. Vinara hao Ruvu Shooting leo watakuwa nyumbani uwanja wa Mabatini, Mlandizi kumenyana na timu inayoshika nafasi ya pili Mji Njombe yenye pointi 19.Aidha Lipuli itacheza na JKT Mlale katika uwanja wa Wambie Iringa, maafande wa JKT Kanembwa wakiwakaribisha Mbao FC katika uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.Kwa upande wa timu za kundi C, vinara Geita Gold wenye pointi 17 wataikaribisha Polisi Mara kwenye uwanja wa shule ya Nyankumbu mjini Geita, JKT Oljoro watacheza dhidi ya Rhino Rangers kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha, huku maafande wa Polisi Tabora wakiwakaribisha Panone FC katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.Kesho kutakuwa na mchezo kati ya African Lyon dhidi ya Kiluvya United kwenye uwanja wa Karume, huku timu ya Manispaa ya Kinondoni (KMC) wakicheza dhidi ya Friends Rangers katika uwanja wa Mlandizi Mabatini.
4