text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
Azam iliyoanza vizuri msimu wa Ligi Kuu imebadilika kwa siku za karibuni na wiki iliyopita ilipoteza mechi baada ya kufungwa bao 1-0 na Coastal Union kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.Timu hiyo imepata kipigo hicho siku chache baada ya kutoka Zambia ilipokwenda kucheza michuano maalumu na kufanya vizuri.Kipigo cha Coastal kimeiacha Azam kwenye nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 42, lakini ikiwa pungufu ya michezo miwili.Yanga inayoshika nafasi ya pili ina pointi 43 na imecheza mechi 18 na Simba inaongoza msimamo ikiwa na pointi 45 na imecheza mechi 19. Akizungumza na gazeti hili jana, Hall alisema anapambana kurudisha makali ya kikosi chake baada ya kuona kinabadilika siku hadi siku.“Timu yangu imebadilika kiasi lakini ni kawaida kwenye mpira kuna mambo mengi uchovu, majeruhi na vitu kama hivyo, yapo baadhi ya mambo natakiwa kuyafanyia kazi na nimeshaanza kufanya hivyo,” alisema.“Tutarudi sawa kwani bado tupo kwenye ushindani wa taji hatupo vibaya, tunaimani tutashinda mechi zetu zijazo bila shaka,” alisema.Azam inatarajiwa kucheza na Mbeya City ugenini uwanja wa Sokine Mbeya mwishoni mwa wiki hii.Mechi na City inatarajiwa kuwa ya vuta nikuvute baada ya kuonekana kuzinduka tangu kuwasili kwa kocha mpya Mmalawi Kinnah Phiri ambaye ameahidi kuishushia kipigo Azam. | 4 |
Uchambuzi wa Sebastien Satigui Kufuatia tathmini ya miezi 43, Mamlaka ya Usimamizi waChakula na Dawa nchini Marekani (FDA) mnamo Julai 7 iliagiza uuzaji wa IQOS nchini humo, Philip Morris International’s (PMI) mfumo wa joto wa tumbaku, kama bidhaailiyorekebishwa ya tumbaku. Uamuzi huu wa FDA (Marekani) unaashiria mara ya kwanza kwa shirika hilo kutoa agizo la uuzaji la MRTP(Modified Risk Tobacco Product) mbadala wa sigara wa elektroniki. Mamlakailigundua IQOS kuwa “inafaa kukuza afya ya umma nainatarajiwa kuongeza faida kwenye afya ya watu kwa ujumla.” Wakati FDA haikubali IQOS, uamuzi wake ulifuatilia hakiki yakisayansi ya ukurasa zaidi ya milioni 1 wa ushahidiuliowasilishwa na PMI na uliozingatia tafiti huru. Mamlaka hiyo iliongezea kwamba bidhaa za tumbaku ambazohaziwezi kuwaka kama IQOS hutofautiana na sigara nyinginehivyo kupunguza uwezekano wa mwili kupata kemikalihatarishi. Hii inaambatana na hitimisho la mapema la vyombo vyakisheria na kisayansi, nchini Uingereza, Ujerumani, naUholanzi, ambazo zimegundua kuwa bidhaa hiyo hutoa viwangovya chini vya sumu hatarishi ukilinganisha na sigara kali. Utafiti huo unatambua teknolojia ya kupunguza athari ya”kutokuwasha-moto”, ambayo huwapa wavuta sigara nikotini, huku ikipunguza sana hatari zinazohusiana na muwako wasigara ya kawaida. Kwa kuzingatia kuwa uvutaji wa sigara unaua watu zaidi yamilioni saba ulimwenguni kila mwaka, uamuzi wa USDA unafungua fursa ya afya ya umma katika mapambano dhidi yajanga la tumbaku ulimwenguni. Hii ni katika kuhimiza uhamajiwa haraka kutoka kwa sigara kali kwenda kwa njia mbadalakama IQOS – kwa watu wazima wanaovuta sigara ambaowameshindwa au hawataki kuacha – inaweza kuokoa maisha. Uvutaji wa sigara unakua haraka barani Afrika na vifo vinazidikuongezeka. Wakati viwango vya sigara vimepungua katika nchitajiri, viwango hivyo vimekua katika mataifa masikini. Katikakusini mwa Jangwa la Sahara, matumizi ya sigara yaliongezekakwa zaidi ya asilimia 50 kati ya 1980 na 2016. Kati ya vifo vyawatu wazima katika nchi za Kiafrika, vifo hivyo vinasababishwana moshi wa pembeni. Zaidi ya asilimia 60 ni kati ya wanawakeambao wanaishi na hufanya kazi na wavutaji sigara. Masomo sita ya kujifunza kutoka kwa uamuzi wa USFDA namamlaka kama hiyo ya udhibiti huko Ulaya.1. Mbinu thabiti ya kudhibiti tumbaku, ambayo inashutumubidhaa zote za tumbaku kama moja ya kisababishi cha athari kwa afya ya umma, ina nafasi ndogo ya kupunguzamadhara ya sigara katika ulimwengu wa leo;2. Mamlaka za udhibiti zinazotegemea utafiti unaotambuateknolojia mpya za kupunguza madhara zinaweza kusaidiakuunda sera madhubuti za umma kupunguza hatari zakuvuta sigara;3. Sekta ya tumbaku lazima iende haraka katika kukomeshautengenezaji na kuuza sigara za kawaida;4. Inapaswa kupunguza gharama ya bidhaa zinazopunguzahatari na kurahisisha upatikana wake kwa wavutaji sigarawatu wazima barani Afrika;5. Nchi zinapaswa kuzingatia kupunguza uharibifu katika safuyao ya hatua za kudhibiti tumbaku na kushirikisha tasnia yatumbaku ili kupata njia bora za kufanya bidhaa mpyazipatikane kwa watu wazima wanaovuta sigara hawafai au hawataki kuacha, ikijumuisha ushuru kwenye sigara zakawaida, wakati kuzipunguza kwa kiasi kikubwa kwenyebidhaa zilizopunguzwa hatari;6. Katika Afrika nzima, ambapo umri wa wastani ni chini yamiaka 25, hatua madhubuti lazima zifanywe ili kuwalindavijana wenye umri wa chini kutoka kwa kupata bidhaampya, kwa kuzingatia kwamba wameonyeshwa mbadalabora lakini ambao sio kwamba hauna hatari kabisa. Katika ulimwengu mzuri, wanadamu wangeepuka vitu vyotevisivyo vya lazima ambavyo vina athari mbaya kwa afya zao. Kwa bahati mbaya, sivyo ilivyo na labda hautawahi kuwa hivyo. Inahitaji ujasiri na utashi wa kisiasa, lakini ni muhimu kwamamlaka za afya ya umma kuchukua hatua za kupunguza hatarikwa wavutaji zaidi ya bilioni moja ulimwenguni. | 0 |
WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imependekeza katika mwaka 2019/20 kufutwa kodi, tozo na ada 10 ambazo zimekuwa kero kwa wadau wa sekta ya mifugo nchini.Akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo bungeni, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesema wizara imefanya tathmini na mapitio ya orodha ya kodi, tozo na ada zinazotozwaAlisema kodi, tozo na ada hizo zinatozwa na wizara ya mifugo na uvuvi, taasisi zake na wizara nyingine chini ya sheria mbalimbali za mifugo na kubaini baadhi ya kodi, tozo na ada hizo ni kero kwa wafugaji na maendeleo ya sekta ya mifugo kwa ujumla.Alisema katika mwaka 2019/20, wizara imetoa mapendekezo ya kuziboresha ili kuondoa usumbufu kodi, tozo na ada kwa wafugaji na hivyo kuongeza mapato katika sekta ya mifugo na kutoa huduma za mifugo kwa wafugaji.Mpina alisema jumla ya tozo 10 zimependekezwa kufutwa, ikiwa ni pamoja na tozo nne za maziwa, tano za nyama na moja ya kuku.Alizitaka tozo hizo za kwenye sekta ya maziwa ni vibali vya chombo cha usafirishaji maziwa chini ya lita 51, usajili wa vituo vya kukusanya maziwa chini ya lita 201, usajili wa wazalishaji wa maziwa chini ya lita 51 na usajili wa wasambzaji wa pembejeo za maziwa.Tozo zinazopendekezwa kufutwa katika sekta ya nyama ni za usajili wa wafugaji wa mifugo ya nyama wadogo, wa kati na wakubwa, usajili wa wasimamizi wa minada ya awali, upili na mipakani na usajili wa minada ya awali na upili na mipakani.“Pamoja na usajii wa wafanyabiashara wa mifugo katika minada ya awali, upili na mipakani, usajili wa wafanyabiashara za nyama na bidhaa za nje ya nchi na vibali vya kusafirisha kuku ndani ya nchi,” alisema.Alisema kumekuwepo na mwingiliano wa majukumu, sheria na kanuni na tozo kati ya wizara hiyo na nyingine, hali ambayo imesababisha urasimu katika utoaji wa vibali na leseni katika ujenzi wa viwanda na uanzishwaji wa biashara.tozo umesababisha ongezeko la gharama za uwekezaji na uendeshaji wa biashara na hivyo kuwepo kwa malalamiko makubwa kutoka kwa wawekezaji na wafanyabiashara.Kutokana na mwingiliano huo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alitoa agizo la kuzitaka wizata tano na taasisi zake kutatua changamoto hizo.Alisema wizara hiyo ilishiriki katika majadiliano na Wizara ya Ujenzi, Viwanda, Afya, Elimu na Kilimo, aidha katika majadiliano hayo taasisi zilizohusika ni pamoja na Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Viwango (TBS), Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) na Wakala wa Taifa wa Barabara (Tanroads).“Majadiliano hayo yanaendelea kwa kuzingatia vigezo muhimu vilivyoanishwa kwenye majukumu ya wizara, muundo, sera, sheria nakala za awali, weledi, viwango na utendaji bora wa kimataifa, jukumu la kiutendaji, kiusimamizi na kiungalizi kwa lengo la kuondoa kasoro zilizopo.”Waziri Mpina alisema utatuzi wa changamoto hizo utapunguza urasimu wa upatikanaji wa vibali na leseni na kupunguza gharama za uwekezaji na uendeshaji wa biashara, kuvutia uwekezaji, kupanua sekta binafsi, kukuza ajira na ukuaji wa uchumi nchini. | 3 |
MOSCOW, URUSI WATU 41 wamekufa baada ya
ndege ya Shirika la Ndege la Aeroflot kutua kwa dharura kabla ya kulipuka na
kutekea moto kwenye Uwanja wa Ndege wa Sheremetyevo, Moscow. Video katika mitandao ya jamii
zinaonyesha baadhi ya abiria wakitumia mlango wa dharura kutoka kwenye ndege
hiyo iliyokuwa ikiteketea moto baada ya kutua vibaya. Watoto wawili na mhudumu
mmoja ni miongoni mwa waliokufa kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Urusi. Shahidi mmoja amesema
ilikuwa ‘miujiza’ kuona kuna walionusurika katika mkasa wa ndege hiyo iliyokuwa
imebeba abiria 73 na wafanyakazi watano. “Watu 37 wamenusurika
ambao ni abiria 33 na wafanyakazi wanne,” alisema mmoja wa maofisa wa
kamati ya uchunguzi wa ajali hiyo, Yelena Markovskaya. Aeroflot lilisema ndege
hiyo ililazimika kurudi uwanjani kutokana na sababu za ufundi
lakini halikufafanua. Awali, ndege hiyo aina ya
Sukhoi Superjet-100, iliondoka uwanja hapo saa 12:02 jioni kwa saa za hapa. Marubani wakatoa tahadhari
ya wasiwasi baada ya kushuhudia hitilafu muda mfupi baada ya ndege kuruka. Baada ya kutua kwa dharura,
huku sehemu za nyuma zikigusa ardhi, injini za ndege hiyo ziliwaka moto kwenye njia
kuu ya ndege, Aeroflot lilisema katika taarifa. Maofisa hao wa ndege
“walijitahidi kadri ya uwezo wao kuwaokoa abiria,” waliofanikiwa
kutolewa katika sekundi 55, shirika hilo la ndege limeeleza. Taarifa pia zinaonyesha
ndege hiyo haikufanikiwa katika jaribio la kwanza la kutua kwa dharura. Kaimu Gavana wa mji eneo
hilo la Murmansk, Andrey Chibis alisema familia za waliofariki duniua katika
mkasa huo watalipwa dola 15,300 kila mmoja, huku waathirikwa watatibiwa katika
hospitali na watapewa dola 7,650 kila mmoja. Mmoja wa abiria, Mikhail
Savchenko anasema alikuwa ndani ya ndege hiyo wakati ikiwaka moto, lakini alifanikiwa
kuruka nje. Alituma video ya abiria
waliokuwa wakihaha kutoka kwenye ndege na kuandika ujumbe: ‘niko sawa, niko hai
na salama.’ Mmoja wa manusura, Dmitry Khlebushkin, amesema
anawashukuru wahudumu wa ndege hiyo kwa msaada wa hali na mali kuhakikisha
wanatoka salama. Uchunguzi umeidhinishwa
sasa kufahamu zaidi kuhusu mkasa huo, taarifa zinasema. | 2 |
Na Nathaniel Limu-Ikungi
WAFANYABIASHARA wa asali wilayani Ikungi mkoani Singida, wanaoendesha shughuli zao kando mwa barabara kuu ya Singida-Dodoma, wamepewa muda wa mwezi mmoja kuanzia sasa kutumia vifungashio halisi badala ya chupa za konyagi ili kulinda afya za walaji.
Agizo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu, alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa matumizi sahihi ya vifungashio vya asali iliyofanyika katika Kijiji cha Issuna wilayani humo.
Alisema ufungashaji wa asali unaofanywa na wafanyabiashara wa asali katika Wilaya ya Ikaungi, si wa kuridhisha na kwa namna moja au nyingine unachangia kuharibika kwa asali.
“Ufungashaji unaofanywa na wafugaji wetu wa nyuki unachangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa soko la asali. Wafanyabiashara hawa wanaouza asali pembezoni mwa barabara wanafungasha asali bila kuzingatia sheria na kanuni za biashara ya mazao ya nyuki hususani asali. Nawapeni mwezi moja mbadilike katika ufungashaji,” alisisitiza Mtaturu.
Mkuu wa wilaya hiyo amewataka wafanyabishara hao wa asali kufanya shughuli zao ndani ya jengo maalumu la kuuzia mazao ya nyuki ambalo tangu lilipomalizika kujengwa mwaka 2013 hadi sasa halijawahi kutumiwa.
Awali Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Wilaya ya Ikungi, Samson Lyimo, alisema asilimia 70 ya eneo la ardhi ya Wilaya ya Ikungi ni misitu, miti, vichaka na nyanda za nyasi au mbuga ambayo ni rasilimali muhimu kwa ufugaji wa nyuki.
“Ufugaji wa nyuki Wilaya ya Ikungi unafanywa na mtu mmoja mmoja na wengine wamejiunga katika vikundi na kufanya shughuli kwa pamoja. Hadi sasa tunavyo vikundi 63 ambavyo vimesajili na vinajihusisha na uzalishaji wa mazao ya nyuki ambayo ni asali na anta,” alisema Lyimo. | 3 |
Na ELIYA MBONEA-MANYARA
BAADHI ya wakulima wa Kata ya Tumati na maeneo ya Mamaisara wilayani Mbulu mkoani Manyara, wameonyesha nia ya kuanza kulima zao la biashara la pareto kwa wingi, baada ya kuhakikishiwa soko la uhakika. Wakulima hao wakizungumzia kuhusu nia ya kurejea kulima zao hilo hivi karibuni wilayani humo, walisema waliamua kuachana na kilimo hicho kutokana na kutoona faida yake hasa katika soko. Akizungumza kwa niaba ya wakulima wenzake, Mkazi wa Kata ya Tumati, Zacharia Boay, alisema uhamasishaji uliofanywa umewapa ari mpya ya kurejea kulima zao hilo la kibiashara. “Wakulima wengi eneo hili kwa hakika wamekuwa na hamasa kubwa ya kuanza kulima tena zao la pareto, baada ya viongozi wa halmashauri kuwahakikishia uwepo wa soko la uhakika tofauti na awali,” alisema Boay. Mkulima huyo aliwataka wakulima wenzake katika maeneo hayo kuhakikisha wanaitumia fursa hiyo ya kilimo cha pareto kujiongezea kipato badala ya kuendelea kulima mazao ya chakula pekee. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga, alisema Serikali wilayani humo itahakikisha inawasaidia wakulima kufikia malengo yao ili wapate faida iliyopo kwenye kilimo. “Tumejipanga kuhakikisha wataalamu wa zao la pareto wanawezeshwa ili wawasaidie wakulima kufikia malengo yao ya kuvuna mazao mengi na yenye tija. “Pareto inayozalishwa kwenye maeneo ya Wiyala yetu ya Mbulu, ni bora kabisa duniani ikiwa inazidiwa tu na pareto inayozalishwa nchini Australia,” alisema Kamoga. Mbali na kuwahimiza wakulima wilayani humo kulima zao hilo, Kamoga aliwataka pia wawekezaji kutoka nje ya wilaya kwenda kuwekeza katika kilimo hicho. | 3 |
TIMU ya Taifa ya Tanzania ya soka la watu wenye ulemavu, ‘Tembo Warriors’ leo inashuka dimbani kucheza na Nigeria katika mchezo wa nusu fainali ya mashindano ya Afrika (Canaf) yanayofanyika nchini Angola. Tembo Warriors imefuzu kucheza nusu fainali baada ya kuifunga Cameroon kwa mabao 7-0 na kufikisha pointi tano katika msimamo wa mashindano hayo ambayo yalichezwa kama ligi kwa sababu yanashirikisha timu sita pekee. Katika mchezo huo, mchezaji wa Tembo Warriors, Khalfan Kilyanga, alifunga mabao manne na kuwa mchezaji wa kwanza kufunga hat-trick, huku Salehe akifunga mabao mawili katika mashijndano hayo. Hadi kufuzu nusu fainali, Tembo Warriors ilicheza michezo mitano na kushinda miwili, dhidi ya Sierra Leone 2-0, dhidi ya Cameroon 7-0, suluhu na Nigeria na kufungwa na Liberia 2-0 na Angola ikaifunga 5-0 Nigeria wanaongoza wakiwa na pointi 11 katika michezo mitano sawa na Angola yenye pointi 11, Tanzania ina pointi saba sawa na Liberia na katika nusu fainali nyingine Angola watacheza na Liberia. Akizungumza kwa njia ya mtandao jana, Rais wa Shirikisho la Soka la Watu Wenye Ulemavu (TAFF), Peter Sarungi, alisema ana amini mchezo wa leo utakuwa wenye ushindani, kwani katika mchezo wa awali waliocheza na Nigeria walitoka suluhu, hivyo kila timu itaingia na mbinu ya kutafuta ushindi ili kufuzu fainali. Nchi zinazoshiriki mashindano hayo ni wenyeji Angola, Liberia, Sierra Leone, Nigeria, Cameroon na Tanzania. | 4 |
Haya yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene Meza, katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.Alitoa mfano kuwa ingawa kuna ongezeko la bei katika vifurushi vya kupata huduma mawasiliano, bado katika kifurushi cha gharama ya chini ambayo ni shilingi 500, mteja anaweza kupata MB za kutosha kutumia intaneti, ikiwemo kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS).Alitoa mfano kuwa mteja akinunua kifurushi cha Sh 500, kati ya hizo fedha Sh 138 inakwenda serikalini kwa ajili ya kodi na kampuni kubakia na Sh 362 ambapo fedha hizo zinamwezesha kupata muda wa dakika 15 za maongezi, ikiwa kila dakika inatozwa Sh 24 , MB za kuperuzi intaneti 8 kila MB ikiwa inatozwa Sh 5 na kutuma ujumbe wa maneno (SMS) 250, ambapo kila ujumbe anatozwa Sh 0.12.“Viwango vya malipo kwa Vodacom ni vya gharama nafuu na vimepangwa kulingana na mahitaji ya wateja wetu licha ya mabadiliko madogo katika bei yaliyofanywa hivi karibuni. Hivi sasa tunatoza Sh 4.9 kwa kila MB katika kifurushi cha GB5 ambapo bei ya awali kilikuwa kinatozwa Sh 3.9 .Bado malipo ya sasa ni madogo ukilinganisha na mallipo yanayotozwa kwenye kifurushi cha GB5 kwenye soko la huduma za mawasiliano kwa fedha za kitanzania kwa mfano Nigeria inatoza Sh 17 Afrika ya Kusini Sh 3, Kenya Sh 12, Ghana Sh 7 na India Sh 5." | 5 |
NAIROBI, KENYA MAHAKAMA ya juu nchini Kenya jana iliionya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) irekebishe kasoro zilizochangia kuufuta uchaguzi wa urais wa Agosti 8, vinginevyo haitasita kufuta uchaguzi ujao wa marudio. Wakati Septemba Mosi, Jaji Mkuu David Maraga alipotangaza kufuta ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta akieleza kwa ufupi sababu za kufanya hivyo, jana alisoma hukumu kamili juu ya sababu zilizowafanya majaji wanne kufuta matokeo hayo. ”Hukumu hii inapaswa kuwa fundisho kwa IEBC kujitazama na kurekebisha makosa na iwapo kasoro zitajirudia, hukumu kama hii itatolewa tena bila kusita,” alisema. Katika maelezo yao Maraga, naibu wake Philomena Mwilu na Jaji Isaac Lenaola, walieleza kubaini kiwango cha kasoro na ukosefu wa uhalali wa matokeo kuwa mkubwa na wa makusudi. Walisema walifuta uchaguzi wa urais baada ya Tume kushindwa kujibu hoja zinazotokana na ushahidi uliowasilishwa na muungano wa upinzani wa NASA uliofungua kesi hiyo. “Ni wazi kasoro zote hizi na nyingi zilitosha kuathiri uhalali wa uchaguzi wa urais,” Jaji Maraga alisema. Pamoja na kwamba matokeo ya urais yalikuwa yakioneshwa katika televisheni, majaji walisema IEBC ilishindwa kuufahamisha umma yanakotoka matokeo hayo na kusisitiza matokeo ya uchaguzi si kuhusu namba. “Kwa upande wetu, uchaguzi si kuhusu namba; matukio, bali mchakato halali wa kidemokrasia,” majaji walisisitiza. Walimtuhumu Mwenyekiti wa Tume, Wafula Chebukati kwa kutangaza matokeo ya mwisho bila uwapo wa fomu namba 34A kitendo ambacho ni ukiukaji wa Sheria ya Uchaguzi. Tume iliendesha uchaguzi wa urais usio halali, usiothibitishwa na wenye uwazi kidogo, majaji walisema. “Kati ya ‘Fomu 34 Bs’ 290 zilizotumika kutangazia matokeo ya urais, 56 kati yao hazikuwa na alama za usalama. Alama za usalama zilipotelea wapi?” alihoji Jaji Maraga. Majaji waliona kuwa kushindwa kwa tume kuwa wazi kukaguliwa kwa mtambo wa kusambaza matokeo licha ya kutumia mabilioni ya dola za walipa kodi kulikuwa uthibitisho kuwa Tume ilificha kitu. “Agizo letu la kuitaka iwaachie wapinzani kukagua mtambo lilikuwa fursa nzuri kwa IEBC kuishinda hoja ya mlalamikaji, lakini waligoma hata kutii agizo la mahakamar” alisema Jaji Mwilu. Aidha alisema mawakili wa utetezi wa IEBC waliupotosha mhimili wa mahakama na kuwaacha majaji bila chaguo jingine zaidi ya kukubiliana na mlalamikaji kuwa uchaguzi ulichakachuliwa. Aidha Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati anapaswa kuwajibika kwa kushindwa kueleza kwanini matokeo ya urais hayakusambazwa kwa namna inavyotakiwa kikatiba. Mahakama inasema IEBC ina wajibu wa kuhakikisha mfumo wa kupiga kura, kuhesabu na kujumuisha matokeo unakaguliwa na u sawa. | 2 |
Akizungumza hivi karibuni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba Tanzania (TCB) , Gabriel Mwalo, amesema kuna faida nyingi katika kilimo cha mkataba lakini kukosekana kwa usimamizi na kutoungwa mkono vya kutosha kutoka serikalini kunawafanya wawekezaji kutochangia fedha nyingi zinazohitajika.Semina hiyo ilikuwa ya kuwaelimisha wahariri na waandishi kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusu manufaa ya kilimo cha mkataba.Alisema upinzani unaofanywa na baadhi ya wadau na wakulima kutokana na maslahi binafsi ambayo ni ya wachache lakini bado kilimo hicho kina tija na ahueni kwa wakulima.Amesema sasa wakati umefika kwa serikali kuyaangalia matatizo yanayokwamisha kilimo cha mkataba na mkazo uwekwe kwenye uzalishaji wa pamba pasiwepo ucheleweshaji wa utekelezaji wa sera ya Serikali.“Sekta ya pamba, kupitia msaada wa Serikali, wasindikaji na wawekezaji, ina fursa ya kufanya maendeleo kwa wakulima kwa ujumla na inaendana vizuri na ahadi ya Serikali ya maisha bora kwa kila Mtanzania.Kama Serikali, inapaswa kuingilia kati na kuweka mazingira yatakayohakikisha kunakuwepo na maendeleo na mkulima kuwa endelevu pamoja na kilimo cha mkataba kwa ujumla.“Wawekezaji wakubwa wanahitaji wakulima wanaoweza kuwasambazia pamba zitakazotumika kwenye vinu vyao, huku wakulima nao wanahitaji wawekezaji kuwapa mitaji kuendesha mashamba yao na kuongeza mavuno. “Kama Serikali inaingilia kati na kusimamia vizuri kilimo cha mkataba, basi kitakuwa na mafanikio makubwa sana zaidi ya ilivyo sasa ,” alisisitiza Mwalo.Ameongeza kusema kwamba hivi leo ekari moja huzalisha kuanzia kilo 250 mpaka 300 za pamba na kama kilimo cha mkataba kitaungwa mkono ipasavyo na Serikali na matatizo machache ya msingi kushugulikiwa, panaweza pakawepo na mavuno kuanzia kilo 1,200 mpaka 1500 kwa ekari moja. | 5 |
Na ABRAHAM GWANDU-ARUSHA HATIMAYE Bunge la Afrika Mashariki (EALA), limemchagua Martine Ngoga kutoka Rwanda kuwa Spika wake na kuwabwaga wapinzani wake Adam Kimbisa kutoka Tanzania na Leontine Nzeymana wa Burundi. Hatua hiyo sasa inahitimisha malumbano yaliyodumu kwa muda wa siku mbili, kuhusu uhalali wa nani anapaswa kuwa Spika kwa mujibu wa kanuni zinazounda Bunge hilo. Uchaguzi huo uliofanyika jana mjini hapa, awali ulitawaliwa na malumbano makali huku baadhi ya wabunge wakitaka kuahirishwa kwa mkutano huo kutokana na kutotimia kwa akidi kwa mujibu wa utaratibu. Kabla ya kuanza kwa uchaguzi huo, baadhi ya wabunge walitaka ufafanuzi wa kina wa kwanini Tanzania na Burundi zimeweka wagombea hali ya kuwa si zamu yao kuongoza chombo hicho. Katika mkutano huo wa jana, wabunge wa Burundi hawakuhudhuria, huku Tanzania waliohudhuria walikuwa wabunge wawili ambao ni Dk. Ngwaru Maghembe na Dk. Abdulah Makame. Aliyekuwa wa kwanza kuhoji uhalali wa kikao hicho kutokana na kutotimia kwa akidi, alikuwa ni mbunge Dk. Ngwaru, ambaye alishauri kuahirishwa kwa kikao hicho. “Ndugu Katibu kutokana na makubaliano miongoni mwa nchi wanachama, kila jambo litafikiwa kutokana na makubaliano na kuzingatia akidi, lakini humu ndani sisi Tanzania tuko wawili na Burundi hawapo kabisa, hatuwezi kufanya chochote kwa mujibu wa sura ya sita ya hati ya makubaliano,” alisema Dk. Ngwaru. Hoja hiyo ya Dk. Ngwaru iliibua malumbano makali, huku Mbunge kutoka Uganda, Suzani Nakawuki alitumia lugha kali na kudai kwamba wabunge kutoka Tanzania na Burundi wako Arusha kwa ajili ya kula chakula cha bure na posho zinazotokana na kodi za wananchi. “Hapa tusilete ubabaishaji, kila nchi ilichagua wabunge kuja hapa kuwakilisha nchi zetu. Mleta hoja anasema hawapo wakati tangu jana tunawaona wakifurahia chakula cha bure na nina hakika wamechukua posho. Mimi naomba tufuate utaratibu, hiki ni chombo huru kisiingiliwe na yeyote,” alisema Nakawuki. Baada ya hoja hiyo, Katibu wa Bunge hilo, Keneth Madete, aliwahesabu wajumbe waliokuwapo ukumbini na kufikia 36 na kuruhusu kuendelea na utaratibu wa uchaguzi wa Spika wa Bunge na kumwita mgombea Ngoga wa Rwanda ili aweze kujieleza kwa wabunge na kuomba kura. Alipomaliza aliwaita wagombea Adam Kimbisa (Tanzania) na Leontine Nzeymana (Burundi) ili nao waombe kura, lakini hawakuwapo ukumbini. | 3 |
Na ABRAHAM GWANDU
-ARUSHA.
CHAMA cha Mapinduzi Mkoa wa Arusha inadaiwa kimewafukuza uanachama baadhi ya vigogo wake akiwamo Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Arusha, Wilfred Soileli.
Wanachama hao wanatuhumiwa kukisaliti chama hicho kabla na baada ya uchaguzi mkuu wakidaiwa kuwa wafuasi watiifu kwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
Wengine waliotimuliwa ni Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa kutoka jimbo la Arumeru Magharibi Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC ) na mfanyabiashara maarufu wa madini ya vito, Mathias Manga na Julius Mungure wa Jimbo la Arumeru Mashariki.
Wakati vigogo hao mkoani Arusha ikielezwa wamevuliwa uanachama wiki iliyopita, Kamati ndogo ya Maadili ya CCM iliyokutana Dodoma iliwahoji wanachama wake ambao wanadaiwa kukisaliti chama hicho.
Hao ni Profesa Juma Kapuya, Nazir Karamagi na Ally Sumaye ambao wote wanadaiwa kukisaliti chama wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Wana CCM hao waliohojiwa na kamati hiyo iliyoongozwa na Naibu Katibu Mkuu Bara, Rodrick Mpogolo, ambaye gazeti hili lilipomtafuta kwa simu, haikupokewa.
Taarifa zilizosambaa jijini hapa jana jioni zilidai uamuzi wa kuwafukuza uanachama viongozi hao ulifanyika katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Arusha kilichofanyika Jumamosi chini ya Mwenyekiti wa chama wa mkoa huo, Lekule Laizer.
Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho waliiambia MTANZANIA kuwa Soileli na Manga walituhumiwa kushirikiana kutoa siri na mikakati ya chama na kuipeleka kwa viongozi wa Ukawa hasa Lowassa ambaye alikuwa mgombea wa nafasi ya Rais.
“Hawa walionywa mara nyingi waache tabia ya kushirikiana na wapinzani hasa Lowassa lakini Manga aliwahi kusema yuko tayari kuchukuliwa hatua lakini asingeacha urafiki wake na Lowassa kwani siasa siyo uadui,” alisema mmoja wa wajumbe wa kikao hicho ambaye hakutata kutwa jina lake gazetini
Gazeti hili lilimtafuta kwa njia ya simu Mwenyekiti Soileli aweze kutoa ufafanuzi wa suala hilo.
Alisema kwa kifupi kuwa bado hajapata taarifa yoyote kuhusu kufukuzwa kwake.
Kwa upande wao wajumbe wa NEC waliofukuzwa uanachama, Mathias Manga na Julius Mungure simu zao hazikupatikana .
Akizungumzia taarifa hizo, Katibu wa Siasa na Uenezi wa Mkoa wa Arusha, Shaban Mdoe, hakukataa wala kukubali ukweli wa taarifa hizo.
Alisisitiza kuwa chama hicho kitatoa ufafanuzi wa kina kuhusu kilichoamuliwa na kikao leo saa 6.00 mchana katika ofisi za CCM Mkoa.
“Siwezi kusema chochote kwa sasa kuhusu taarifa hizo mpaka kesho Jumatatu saa 6.00 mchana.
“Hizo tetetsi zinazosababisha maswali kuhusu uamuzi uliofikiwa na kikao cha Halmashauri Kuu ya Mkoa kilichoketi Jumamosi tutatoa ufafanuzi kesho Jumatatu (leo),” alisema Mdoe. | 3 |
Na Mwandishi Wetu- Dodoma
SERIKALI imeziagiza halmashauri, miji na majiji nchini kutoa kipaumbele cha ajira kwa wahitimu wa Chuo Kiongozi cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa (LGTI).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene, amesema hivi karibuni kuwa Chuo Kiongozi cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa (Hombolo) kipo mahususi kwa kutoa mafunzo kwa ajili ya wafanyakazi wanaoajiriwa kwenye Serikali za mitaaa nchini.
“Naagiza kunapokuwa na nafasi za kazi kwenye halmashauri, miji na hata majiji ni vyema wahitimu wa chuo hiki wakapewa kipaumbele. Ni vizuri wakapata nafasi ya kushindanishwa na wengine kwani hawa ni walengwa,” alisema Waziri Simbachawene wakati alipokutana na viongozi na wawakilishi wa chuo hicho mjini Dodoma.
Waziri Simbachawene aliuagiza uongozi wa chuo hicho kutosita kutoa taarifa yoyote endapo chuo kinapokuwa na upungufu wa watumishi.
Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Martin Madale, alimshukuru Waziri Simbachawene kwa kuwa karibu na chuo na pia kufuatilia maendeleo na ustawi.
“Kwa niaba ya bodi, menejimenti, wafanyakazi na wanachuo wote wana imani kubwa na uongozi wako kwani umekuwa karibu sana nasi na pia umekuwa msaada mkubwa katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazokikabili chuo,” alisema Dk. Madale.
Alimwomba waziri kukisaidia chuo kupata kompyuta zaidi, viti na vifaa mbalimbali ili kukabiliana na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaoomba kujiunga na chuo hicho kwa sasa. | 3 |
Kamishna wa Madini nchini, Paul Masanja aliyasema hayo mjini hapa jana wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na wizara yake.Maswi, ambaye alisema lipo ongezeko la hazina ya madini hayo nchini, alisema kituo hicho kitakuwa na huduma zote muhimu zikiwemo za kibenki zitakazowawezesha wachimbaji na wafanyabiashara kutokutafuta huduma muhimu zinazoendana na shughuli hizo nje ya kituo hicho.“Shughuli zote za uuzaji na ununuzi madini ya vito na usonara zitafanywa katika kituo hicho, kutakuwa pia na helkopta itakayotua moja kwa moja katika jengo hilo jambo ambalo litawezesha uwepo wa usalama katika biashara nzima ya kuuza na kununua madini.“Tunataka kupitia sekta ya madini kuiwezesha serikali kuongeza mapato yake na kutoka hapa tulipo kiuchumi.“Jambo hilo linawezekana ndio sababu tunaanza na kuboresha sehemu za kazi ili kuwawezesha watumishi kufanya kazi katika mazingira mazuri zaidi na kuongeza uwajibikaji,” alisisitiza Masanja. | 5 |
Na ASHA BANI-DAR ES SALAAM MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha amekiri wazi kwamba siasa zimeharibu utengamano wa wanannchi, huku akiwataka wanasiasa visiwani humo kupunguza jazba ili waijenge nchi yao. Jecha aliyasema hayo jana katika kipindi cha Funguka kinachorushwa na Televisheni ya Azam, kilichoongozwa na Mtangazaji mkongwe, Tido Mhando. Pamoja na mambo mengine, Jecha alisema kutokana na jazba hizo, itachukua muda mrefu kwa Zanzibar kujenga maelewano ya kindugu. Tido: Unafikiri nini kifanyike ili Zanzibar iweze kuwa na utulivu na watu kukaa pamoja bila chuki. Jecha: Kinachotakiwa watu tupunguze jazba ya kisiasa tukae tukubaliane na tujenge nchi yetu, lakini kutokana na jazba hizi itachukua muda sana katika hili. Tido: Unaponambia jazba ya kisiasa nakuelewa lakini kulikuwa na maridhiano ila matokeo ya uchaguzi uliopita yameondoa maridhiano hayo kabisa. Jecha: Matokeo yaliyopita hayajaondoa maridhiano kwani yapo kwenye Katiba lakini utaratibu wake ndio uliovurugika kidogo. “Na hii jazba ya kisiasa imesababisha hadi watu hawaendi kuzikana kabisa, ndio imefika hapa tulipo sasa kikubwa waondoe jazba na ndio itatufikisha mbali katika maendeleo ya kujenga nchi. “Ndugu hawaongei, hawasalimiani, jamii haziabudu pamoja wala haziwi huru, wanaogopa, watu hawafanyi huduma za kijamii hata kwenye gari za abiria watu wanasusiwa hii haipendezi ,’’alisema Jecha. Aliongeza kwa kuhoji kuwa ni kwa sababu gani mazao ya watu katika visiwa vya Pemba yanaharibiwa hii haijawahi kutokea, nyumba zinachomwa moto, mifugo inauliwa jambo ambalo si ubinadamu. “Jaziba za kisiasa ndugu hawaongei ni uhasama , mtangazaji uje zanzibar utembee usikie watu wanavyoishi kwa sasa. Tido : Huoni hali hiyo inatokea kwa sababu kuna hali ya ung’ang’anizi kwamba upande mmoja unashindwa lakini kila siku hawakubali na wanatumia kila njia kubakia madarakani? Jecha: Hakuna ung’anganizi, uchaguzi ulifutwa, kila chama kilikuwa huru kupeleka majina na kila chama kilishiriki uchaguzi ulikuwa huru, vyama vyote vilishiriki uchaguzi. Tido: Inaonekana ulifuta uchaguzi wakati huo ukiwa na hisia kali. Jecha : Sikuwa na hisia kali ni uchaguzi wa kawaida na umefuata sheria zote hakuna tatizo sikuwa na tatizo. Tido: Lakini ni kitendo kipya si jambo la kawaida Jecha : Uchaguzi wowote unatawalia na sheria na utaratibu na uchaguzi mwaka 2015 ulikwenda sawa lakini kulitokea na vitendo vingi ambavyo havikuwa vya kawaida ndio ukasababisha kufutwa kwa uchaguzi huo. Tido: Ulitaja mambo kadhaa ikiwa ni sababu za kufutwa kwa uchaguzi huo kwa mfano, kufutwa fomu za kura vijana kufanya fujo mtaani, na kutangazwa kwa matokeo mapema.lakini wanasema umetoa sababu hizi wakati watu hawakuyaona huko mitaani na wala hawakuyashuhudia bayana ninyi mkabaini. Jecha: Matokeo hayo yalionekana mapema na baadhi ya vyama vilivyoshiriki uchaguzi vililalamikia hayo mambo yaliyosababisha uchaguzi huo kufutwa. Tido: Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) inamchanganyiko ya wajumbe wa kutoka vyama mbalimbali vya siasa hili unalichukuliaje? Jecha: Hii ni zuri sana lakini ina changamoto hakuna chama kujichukulia mamlaka ndani ya Tume. Na kuna wakati kuna mambo yanaingizwa kivyama zaidi hii ndio inakuwa tabu. Tido : Lakini katika uchaguzi uliopita mambo yalikwenda vizuri,wachunguzi wa mambo walisema hakukuwa na shida, magazeti pia walisema mambo yalikuwa mazuri na hata waangalizi hili lipoje? Jecha: Kulikuwa na mambo mengi sana yaliyokuwa na matatizo kwenye uchaguzi huo na nitayatoa mwezi Februari mwaka huu, tayari tumeandaa taarifa bado wakati wake tu kutoka. Tido : Ulisimamisha uchaguzi lakini watu walijipanga upande pale pale kwenye ukumbi Bwawani, mara wanasikia umeenda kwenye televisheni kutangaza tena peke yako hili lipoje? Jecha: Haya yote yataonekana kwenye taarifa ya uchaguzi na si hapa siwezi kusema sasa hivi. Tido: Je mlifuata utaratibu? Jecha: Utaratibu ulifuatwa na wakati wa matokeo ya Zanzibar hasa Unguja hakukuwa na hitilafu, matatizo yalionekana wazi wazi taarifa zilipoanza kutufikia hasa za kisiwa cha pemba. Ikaonekana kulikuwa na ukiukwaji mkubwa sana na sio kupiga kura ni baada ya kura zilishapigwa kulitokea na utaratibu mbaya. ‘’Kulitokea utaratibu wa kiufundi ukaharibu matokeo ya kura, ikiwa ni pamoja na urekebishaji wa kasoro kulifanyika mambo ambayo hayakutakiwa kufanyika nje ya uchaguzi,’’alisema Jecha. Tido: Kuna watu mnadhani walifanya hivyo? Jecha : Sisi kama tume hatuna watu hao bali Jeshi la Polisi wanayo majina hayo. Tido: Lakini iweje ielezwe kwamba kura zilizoharibika na vurugu ni za Zanzibar na sio serikali ya Muungano, kwamba kura za Muungano zilikuwa shwari? Jecha: Bwana Tido hayo tungeliacha lakini hisia kali haikuwa kwenye muungano kulikuwa na hisia kubwa kwenye kura za Zanzibar. | 3 |
TIMU ya Soka ya Taifa ya Vijana ya Bara chini ya umri wa miaka 20, jana ilitinga fainali za michuano ya Kombe la Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati na sasa itacheza fainali na Kenya mwishoni mwa wiki hii.Tanzania Bara iliingia fainali kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Sudan katika mechi iliyochezwa mjini Gulu, Uganda. Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Pece mjini Gulu, mabao ya Tanzania yalifungwa na Israel Mwenda na Kelvin John dakika ya 39 na 45 huku la wapinzani likifungwa dakika ya 57 na Muhamad Abbas.Kwa upande wa Kenya ilitinga fainali jana kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Eritrea katika mchezo uliofanyika Njeru, Uganda. Tanzania na Kenya zilikuwa kundi moja sambamba na Ethiopia na Zanzibar kwenye kundi B. Fainali hiyo huenda ikawa ngumu kwani katika mchezo wa makundi Tanzania na Kenya zilitoka sare ya mabao 2-2.Kuhusu mchezo huo dhidi ya Sudan awali, Tanzania ilitawala mchezo na kutumia nafasi ilizopata ambapo kipindi cha kwanza walikwenda mapumziko wakiongoza kwa mabao 2-0. Kipindi cha pili Sudan waliingia kwa kasi na kushambulia zaidi dakika za mwanzo na kupata bao huku wachezaji wa Tanzania Bara wakionekana kucheza kana kwamba wamechoka.Kocha wa timu hiyo, Zuberi Katwila aliona hali hiyo na kufanya mabadiliko ya baadhi ya wachezaji yaliyoonekana kurudisha uhai na kasi ambapo licha ya kutoongeza bao walianza kushambulia na kutengeneza nafasi nyingi ingawa hawakuwa makini kuzitumia. Sudan na Eritrea sasa zitacheza mechi ya kuwania mshindi wa tatu mwishoni mwa wiki hii. | 4 |
MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) imesema itafanya uchunguzi ili kubaini sababu za Kampuni ya R& S Inter Trade ya Vingunguti jijini Dar es Salaam, kukutwa na shehena kubwa ya vipodozi vilivyokwisha muda wa matumizi.Meneja wa TFDA wa Kanda ya Mashariki jijini Dar es Salaam, Emmanuel Alfonce alisema hayo alipofanya mahojiano maalumu na gazeti hili kuhusu kampuni hiyo kukutwa na vipodozi hivyo vilivyokwisha muda wake.Chanzo kimoja cha habari kililiambia gazeti hili uwepo wa shehena ya zaidi ya katoni 2,000 za vipodozi vilivyokwisha muda wake katika ghala la kampuni hilo, lililopo Vingunguti jijini Dar es Salaam.Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, kampuni hiyo iliingiza zaidi ya katoni 4,000 za vipodozi vilivyoharibika muda wake katikati ya mwaka jana, lakini baadaye ilibainika kuwa vilikuwa vimekwisha muda wake, ambapo wakaguzi kutoka TFDA waliamuru vipodozi hivyo kuteketezwa.Hata hivyo, pamoja na agizo hilo, ilidaiwa kuwa hadi sasa ikiwa ni zaidi ya miezi sita, bado vipodozi hivyohavijateketezwa, hatua inayodaiwa kuwa inaweza kusababisha udanganyifu kwa vipodozi hivyo kuingizwa sokoni kwa njia zisizo halali.Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja Alfonce alisema pamoja na kufuatilia ili kujua sababu zilizosababisha vipodozi hivyo kushindwa kuteketezwa kwa muda mrefu sasa, lakini pia itafanya uchunguzi kubaini sababu za kampuni hiyo kukutwa na kiwango kikubwa cha vipodozi vilivyokwisha muda wake.“Tutafuatilia kujua ni kwanini kampuni hiyo imeweza kuwa na kiwango hicho ambacho ni kikubwa sana cha vipodozi vilivyokwisha muda wake.“Kuhusu kuviteketeza utaratibu wa vipodozi ni tofauti kidogo na vyakula ambavyo baada ya kuvikamata vikiwa vimeharibika, tunamuamuru aliyekutwa navyo kuvipeleka dampo Pugu chini ya usimamizi wetu.“Kwa vipodozi Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezuia kuvipeleka dampo vikiwa vimekwisha muda wake kwa vile vinaweza kuwa na kemikali zenye athari kwa ardhi na mazingira, kwa hiyo kinachofanyika kwa vipodozi ni kuviteketeza kwa kuvichoma moto na kuna matanuru maalumu ya kuviteketeza,” alisema meneja huyo.Alisema kwa vile wakaguzi wa TFDA walishafika katika maghala ya kampuni hiyo na kuamuru kuteketezwa kwa vipodozi hivyo, watafuatilia ili kuona ni kwanini kazi hiyo haijafanyika hadi sasa.Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Nassoro Abdallah alikiri kuwepo kwa vipodozi hivyo vilivyokwisha muda wake katika ghala la kampuni yake.Hata hivyo Mkurugenzi huyo alikanusha madai kwamba shehena hiyo, imekuwa inapungua bila kujua katoni nyingine zinakwenda wapi, kama ilivyodaiwa na vyanzo vya habari.Alisema ipo shehena kidogo ambayo iliteketezwa, ingawa alishindwa kusema kazi hiyo ilifanyika lini na ilisimamiwa na chombo gani. | 3 |
JESHI la Polisi Wilaya ya Igunga, mkoani Tabora linawashikilia viongozi wanane kwa tuhuma za wizi wa Sh milioni 43 za wakulima.Wanaoshikiliwa wamo Mwenyekiti, Katibu na Meneja wa Chama cha Ushirika katika kijiji cha Imalanguzu kata ya Mwamakona tarafa ya Igurubi kwa tuhuma za upotevu wa Sh milioni 43 za wakulima wa zao la pamba zilizolipwa na kampuni ya OLAM.Ofisa Tarafa ya Igurubi, Judith Haule alikiri viongozi hao kukamatwa na jeshi la polisi huku akiwataja majina yao kuwa ni Mwenyekiti wa AMCOS Gibe Basil, Katibu na Meneja Majila Bundala na viongozi wengine Sali Tano, Mkinga Nzumani, Deus Lusendeka, Jisusi Kadodi, Juma Ali, Samsoni Jidayi wote wakazi wa kijiji cha Imalanguzu.Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamatwa viongozi hao wanane, Haule alisema walibaini kuliwa fedha hizo baada ya kuona baadhi ya wakulima wakiendelea kudai fedha za pamba huku kampuni ya OLAM ikiwa tayari ilishawalipa.“Mimi nilipigiwa simu na mtendaji wa kijiji hicho cha Imalanguzu kuwa kuna viongozi wanane wa AMCOS wamekula fedha za wakulima wa zao la pamba na ndipo niiamua kwenda hadi kijiji hicho.Haule alisema baada ya kufika alishirikiana na Ofisa ushirika wilaya ya Igunga, Michael Mtaturu ambapo baada ya kufanya ukaguzi kwenye vitabu vya malipo wakishirikiana na viongozi hao wanane walibaini kuliwa Sh milioni 43 na viongozi hao.Walipowahoji viongozi hao juu ya fedha hizo walianza kurushiana mpira huku kila mmoja akimtupia lawama mwenzake.Hata hivyo, Haule alibainisha kuwa baada ya kubaini fedha hizo kuliwa na viongozi hao aliamua kutoa taarifa kwa Katibu Tawala Wilaya ya Igunga, Godslove Kawiche ambapo naye aliripoti kwa Mkuu wa polisi Igunga na baadaye viongozi hao kukamatwa.Aidha Ofisa tarafa huyo hakuweza kutaja idadi ya wakulima wa zao la pamba ambao fedha zao zimeliwa na viongozi hao.Fedha hizo zilianza kuliwa kidogo kidogo kuanzia Julai 2019 huku wakulima wakipigwa chenga.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Barnabas Mwakalukwa alipoulizwa juu ya viongozi hao wa AMCOS endapo wanashikiliwa na polisi alisema “mimi nimesikia kama ulivyosikia wewe, lakini taarifa kamili bado haijafika rasmi kwangu ila ikifika nitatoa taarifa kwenye vyombo vya habari”.Hata hivyo hadi jana jioni viongozi hao wa AMCOS walikuwa bado wako mahabusu kwa siku nne huku ikielezwa kuwa hawataachiwa hadi walipe fedha hizo za wakulima walizokula. | 3 |
IDARA ya Misitu na Mali zisizorejesheka imewahamisha watu waliokuwa wakiishi katika eneo la msitu wa Hifadhi wa Kiwengwa Mkoa wa kaskazini Unguja, ili kuepuka athari za uharibifu.Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Mali zisizorejesheka, Soud Mohamed alisema serikali imechukua hatua hizo baada ya kubainika watu waliokuwa wakiishi eneo hilo kufanya vitendo vya uharibifu wa mazingira na ukataji wa msitu.Aliyataja matukio yaliyokuwa yakifanywa katika msitu wa hifadhi wa Kiwengwa ni pamoja na kukatwa kwa baadhi ya miti kwa matumizi ya mbao.''Idara ya Misitu na Mali zisizorejesheka imechukua hatua ya kuwahamisha watu waliokuwa wakiishi ndani ya sehemu ya msitu wa Kiwengwa baada ya kubaini matukio ya vitendo vya hujuma vya uharibifu wa msitu huo,'' alisema.Aidha, alisema idara imejipanga zaidi kuhakikisha baadhi ya misitu ya hifadhi haihujumiwi ikiwemo kukatwa kwa miti yake kinyume na malengo.''Tumeanza mikakati ya kuimarisha ulinzi katika maeneo ya hifadhi ya misitu nchini ili kuepuka uharibifu unaoweza kufanywa na jamii ya wananchi wetu,'' amesema.Ofisa anayeshughulika na masuala ya ulinzi katika msitu wa hifadhi ya Kiwengwa, Ali Juma alisikitishwa na matukio ya uvamizi wa hifadhi ya msitu yanayofanywa na watu wasiokuwa waaminifu.Alisema baadhi ya miti adimu imekuwa ikikatwa kwa ajili ya matumizi ya mbao ikiwemo Msaji.''Ipo baadhi ya miti imeanza kuadimika nchini na imekuwa ikikatwa kwa ajili ya matumizi ya mbao, hivyo kusababisha uharibifu mkubwa wa rasilimali ya taifa,'' amesema.Baadhi ya misitu ya hifadhi ya taifa ambayo imeanza kuhujumiwa na kuvamiwa na wananchi ni pamoja na Kiwengwa, Jozani na Hanyegwa mchana Unguja. | 3 |
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Dunini (WFP), limepokea mchango wa Euro milioni 9.5 kutoka Umoja wa Ulaya (EU) kwa lengo la kuunga mkono mradi wenye thamani ya Euro milioni 24.5 (takribani Sh bilioni 50) kusaidia na kukuza usalama wa chakula na lishe katika mikoa ya kanda ya kati.
Mradi huo umeandaliwa ili kuimarisha usalama wa chakula na lishe kwa watu wapatao 40,000 na wakati huohuo ukichangia katika kupunguza utapiamlo katika wilaya zinazolengwa za Bahi na Chamwino mkoani Dodoma, Ikungi na Singida Vijijini katika Mkoa wa Singida.
Mchango wa EU ulitangazwa jana Dar es Salaam katika hafla ya kusaini makubaliano katika Jengo la Umoja jijini Dar es Salaam uliofanywa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubisya, Mwakilishi wa WFP Tanzania, Michael Dunford na Mkuu wa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Roeland Van De Geer.
“Licha ya kuimarika kwa viashiria vingi vya afya katika muongo uliopita, bado hakuna hatua kubwa katika kuimarisha hali ya lishe ya watoto na wanawake nchini Tanzania.
“Kuwapo viwango vya juu vya kudumaa, kukosa uzito wa kuridhisha na upungufu wa viinilishe nchini kunaashiria dharura ya kimyakimya. Utayari wa kisiasa katika safu ya viongozi wa juu katika kukabili lishe duni nchini Tanzania kwa mtazamo wa sekta nyingi kwa hakika ni mageuzi makubwa.
“Kupitia mradi huu, EU pamoja na WFP ziko katika nafasi nzuri ya kubaini na kuunga mkono uhusiano kati ya kilimo, afya, usalama wa chakula na lishe, ambao hapo kabla haukuwa umeelezwa kwa kina au kufuatiliwa kikamilifu,” alisema Van De Geer. | 3 |
Mwandishi Wetu , MorogoroMwanamuziki wa Mchiriki kutoka kundi la Jagwa Music, Jackson Kazimoto maarufu Jack Simela amezikwa leo Desemba 10, katika makaburi ya Bigwa mkoani Morogoro. Jack amezikwa katika makaburi hayo pamoja na mjomba wake, Ibrahim Karata ambaye ni mtoto wa shangazi yake, Elizabeth Kazimoto aliyezikwa jana katika makaburini hapo. Baba wa msanii huyo, Leonard Kazimoto ameiambia Mtanzania Digital kuwa msanii huyo, mjomba wake na wenzake watano walifariki dunia wakiwa njiani kwenda makaburi ya bigwa kwa mazishi ya shangazi wa msanii huyo. “Wakati tunaenda kuzika tulitoka wote hapa maana msiba ulikuwa Mwembesongo wao walikuwa saba wote waliingia kwenye gari lao dogo walipitia barabara kuu ya Moro/ Dar sisi tulipita barabara ya zamani ya Dar, tulipofika makaburini ilituchukua muda kuwasubiri maana tulitaka Jack amzike shangazi yake na pia Ibrahimu Karata naye amzike mama yake ila tulipoona hawatokei tukazika. “Kumbe walikuwa wamepata ajali eneo la nane nane maarufu kwa jina la Jordan na wote sita wamefariki dunia isipokuwa mmoja amelazwa yupo hoi hospitalini,’’ amesema. Amesema waliporudi nyumbani walishangaa kuona vilio vikizidi walipohoji ndipo wakaambiwa kuna msiba mwingine Jack, Ibrahim na wenzao wengine waliokuwa kwenye gari ndogo waligongana na gari kubwa. Naye shangazi wa msanii huyo, Yasinta Kazimoto amesema alimlea msanii huyo aliyezaliwa 1986 tangu alipokuwa na miaka nane baada ya mama yake mzazi kufariki mwaka 1994. “Nilimlea vizuri hadi mwaka 2004, alipokuja kuchukuliwa na meneja wake, Gola tangu alipomuona alipokuwa akiimba kwenye moja ya maonyesho ya Jagwa Manzese mkoani hapa hadi sasa mauti yemamkuta ameishi katika kundi la Jagwa kwa miaka 13, alikuwa mtu safi alinipa zawadi kila aliposafiri sikupata naye tabu katika malezi yake,’’ amesema Shangazi yake. Ameongeza kwamba msanii huyo ameacha watoto watatu, Saidi (18), Nuru (17) na Leonard (4). Meneja wa mwanamuziki huyo, Abdallah Salehe maarufu meneja Gola amesema kifo cha msanii huyo aliyehitimu elimu ya msingi Shule ya Mwembesongo mkoani hapa ni pigo kubwa kwa tasnia ya muziki wa mchiriku na kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa amebaki kuubeba muziki huo. “Jack ndiye alikuwa amebaki kuubeba muziki wa mchiriku kifo chake ni pigo kubwa kwa muziki huo, kwani uwezo na uvumilivu wake baada ya wasanii wengi kuliacha kundi la Jagwa ndiyo ulikuwa ukibeba kundi hilo kote ndani na nje ya nchi walipokuwa wakifanya maonyesho yao,’’ amesema Gola. Hata hivyo baadhi ya wasanii ambao hawakutaka kutajwa majina yao walishangazwa na wadau wa muziki huo kutokufika katika mazishi ya msanii huyo huku wakiongeza kuwa wajenge utamaduni wa kuzikana, sababu wote njia yao ni moja. | 1 |
MKUU wa Jeshi la Polisi nchin (IGP), Simon Sirro amesema waliohusi- ka na vitendo vya mauaji ya Watanzania 9 baada ya kupigwa risasi na wengine kushambuliwa kwa mapanga na watu wasiojulikana walianza chokochoko hizi eneo la Kibiti mkoani Pwani na walipovurumishwa na jeshi la Polisi, wengine walikimbilia nchi jirani ikiwemo Msumbuji. Watu hao waliuawa na watu aliokuwa wameva- lia sare za jeshi kwenye kijiji cha Mtole kilichopo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pembezoni mwa mto Ruvuma na akasisitiza kuwa watasakwa popote walipo na watachukuliwa hatua za kisheria huku akiwahakikishia Watanzania ulinzi na usalama.IGP Sirro alisema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa Kata ya Kitaya halmshauri ya Wilaya ya Mtwara wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo mara baada ya kutembelea kata hiyo kwa lengo la kusalimiana na kuwapa pole Watanzania hao. Mauaji hayo yalitokea Juni 26 mwaka huu ambapo wanawake watatu na mtoto mmoja wameshikiliwa lakini pia wanawake saba walite- kwa kwa muda wakati wa tukio hilo la mauaji na kisha kuachiwa, huku mmoja kati yao alitumwa ujumbe aje aseme kwa serikali ya Tanzania. Mkuu huyo wa polisi atuma salamu kwa wa- husika wa mauaji hayo kuwa, Tanzania ni nchi yenye amani ila kwa wale ambao hawajazoea amani watapata tabu na kueleza kuwa mchezo huo walianzia maeneo ya Kibiti na kisha baadhi yao kukimbilia Msumbiji.Mtanzania Fatuma Masudi aliyenusurika katika mauaji hayo alipewa ujumbe afikishe kwa serikali ya Tanzania uliokuwa unas- ema: “Tunakupa salamu uende ukasema huko kwenu yakikauka tu maji tunavuka sisi wala hatuogopi nenda kaseme.” Somoe Mkilwa ambaye aliamriwa kuondoka nchini humo na wahusika wa mauaji hayo akitoa ush- uhuda kwa kile kilichotokea alisema, “walinigongea kibandani kwangu wali- kuwa watatu, wakachukua tochi wakamulika mulika wakaniuliza wewe mama uko na nani nikawaambia niko peke yangu, una unga na mchuzi tunataka utupikie ugali nikawaambia sina mchuzi basi wakakuta unga wakachukuwa wakaniambia nenda kwenu hii nchi sio salama.”Hata hivyo serikali ya Tanzania kesho inakutana na serikali ya Msumbiji ili kuweka mambo sawa kufua- tia tukio hilo la mauaji kwa wakazi wa kata hiyo huku watanzania wakitahad- harishwa kutoenda nchini humo kwa sasa hadi hapo hali itavyokuwa shwari. | 3 |
MKURUGENZI wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Rose Reuben ametwaa tuzo ya ‘Wanawake katika Uongozi’ iliyotolewa na World Women Leaders Congress (WWLC), jijini Dar es Salaam. Tuzo hiyo ilitolewa 19 kwa wanawake viongozi wa Afrika Mashariki walioleta mabadiliko katika jamii, walioibua vipaji, wanawake mifano ya kuigwa na wenye uthubutu kutoka taasisi na mashirika binafsi na serikali. Mbali na Rose, mwanamke mwingine aliyetunukiwa tuzo hizo kutoka Tanzania ni Emma Kawawa ambaye Mkurugenzi Mtendaji na mwanzilishi wa Tanzania Women CEO’S Roundtable. Wanawake viongozi kutoka Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi walitunukiwa tuzo hizo kutokana na vigezo vya ushindi vilivyowekwa. Akizungumzia tuzo hiyo, Rose amesema hatua hiyo inawatia moyo wanawake wengine kufanya bidii. “Wanawake wanaweza kuwa viongozi wazuri, tuzo hii inaeleza kuwa uongozi wa wanawake unakubalika, hii ni tuzo ya dunia, kumbe ulimwengu umekubali kuwa wanawake wanaweza kuwa viongozi,” amesema.Ameongeza: “Jamii kwa ujumla ikubali kuwa wanawake wanaweza kuwa viongozi. Wanahabari wafanye kazi zao kwa kujiamini, kazi zao zikajulikana na wasikatisshwe tamaa na kitu chochote.” Tuzo hizo zinatolewa ili kuhamasisha wanawake viongozi katika sekta za umma na binafsi, kutambua mafanikio ya wanawake kikanda na kidunia pamoja na kuwatia moyo wanawake vijana kushika nafasi za mbalimbali za uongozi. | 3 |
['Kiungo wa kati wa Crystal Palace na Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, amepata pigo baada ya uhamisho wake kwenda Everton kutibuka lakini amesisitiza anataka kuondoka Selhurst Park. (Telegraph) ', 'Zaha anahofia amepoteza nafasi ya kuhama kwa kitita kikubwa imepotea baada ya dirisha la uhamisho wa wachezaji kufungwa siku ya Alhamisi. (Mail)', "Meneja wa Palace Roy Hodgson alimzuia Zaha kufanya mazoezi siku ya Alhamisi kwa sababu mchezaji huyo ''hakuwa na utulivu wa kiakili'' baada ya kuwasilisha barua ya kuomba uhamisho. (Mirror)", 'Uhamisho wa mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala,25, kutoka Juventus kwenda Tottenham uligonga mwamba kutokana na changamoto zinazohusiana suala la haki ya picha. (ESPN)', 'Spurs iliomba usaidizi kutoka kwa Juventus kulipa haki ya picha ya Dybala- lakini mabingwa hao wa Italia hawakua wamejiandaa kulipa fedha hizo. (90min)', 'Tottenham wanaamini walikua na £64m kumnunua Dybala, lakini Juventus hawakutilia maanani wazo hilo kwa sababu walikuwa wanamlenga Romelu Lukaku japo kiungo huyo alikuwa na mpango wa kuhamia Inter Milan. (Telegraph)', 'Manchester United ilijiondoa katika mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Juventus na Croatia Mario Mandzukic, 33, baada ya kutoelewana na mabingwa hao wa Italia . (ESPN)', 'Real Madrid wanaamini wamemkosa kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, baada ya United kutoimarisha safu yake ya kati siku ya mwisho wa uhamisho wa wachezaji.', 'Klabu hiyo inayoshiriki ligi ya Uhispania maarufu La Liga, badala yake imeelekeza darubini yake kwa mshambuliaji wa Paris St-Germain na nyota wa kimataifa wa Brazil Neymar, 27. (Marca)', 'Hofu ya kikosi cha kwanza kitakacho cheza chini ya meneja mpya wa Chelsea Frank Lampard imemfanya beki wa Brazil David Luiz, 32, kushinikiza uhamisho kwenda Arsenal. (Standard)', 'Meneja wa Everton Marco Silva alikuwa tayari kuongeza kasi ya katika safu yake ya mashambulizi siku ya mwisho ya uhamisho wa wachezaji na alikuwa namlenga winga wa Arsenal Alex Iwobi, 23 , wa Nigeria akimkosa Zaha. (Guardian)', 'Tottenham walipata pigo baada ya Sporting Lisbon kukataa kupunguza bei ya kiungo wao wa kati Mreno Bruno Fernandes, 24. (Mirror)', 'United ilipuuza nafasi ya kumsajili mshambuliaji Moise Kean kutoka Juventus, kabla ya kiungo huyo wa miaka 19 kujiunga na mahasimu wao Everton. (90min)', 'Lakini Everton hawakua tayari kufikia ofa ya Manchester United ya kumuuza beki wa Argentina Marcos Rojo. (Sky Sports)', 'Rojo alighabishwa sana na hatua hiyo baada ya pendekezo lake kuhamia Everton kutibuka. (Mail)', 'Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Louis Saha anasema uamuzi wa klabu hiyo kusaini beki wa Tottenham na Ubelgiji Toby Alderweireld, 30, wakati wa uhamisho wa wachezaji ni "siri ya ajabu". (MEN)', 'Tetesi Bora Alhamisi', 'Azma ya Barcelona kumsajili tena Neymar, 27, inategemea ikiwa klabu hiyo itamuuza Philippe Coutinho ambaye pia ni mchezaji mwenzake wa kimataifa wa Brazil. (Goal)', 'Kingo wa kati wa Juventus Sami Khedira, 32, amekataa uwezekano wa uhamisho mara mbili kwa sababu anaazimia kujiunga na Arsenal. (Star)', 'Manchester United wako tayari kulipa £81m ambayo itawawezesha kumnyakua mshambuliaji wa Uhispania na Athletic Bilbao Inaki Williams, 25. (El Chiringuito TV - via Mail)', 'Pendekezo la Leroy Sane kuhamia Bayern Munich kutoka Manchester City limeathiriwa na jeraha la goti linalomkabili nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani. (Mail)', 'Atletico Madrid wanajiandaa kumsajili mchezajiwa safu ya kati wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen, 27. (Independent)'] | 4 |
SERIKALI ya Tanzania imesema itaendelea kufanya kazi kwa karibu na kuimarisha uhusiano wake wa muda mrefu na wa kihistoria na Serikali ya Poland kwa faida ya nchi zote mbili.Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwingi wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka 100 ya Uhuru wa Poland zilizofanyika ofisi za ubalozi huo jijini Dar es Salaam juzi.Balozi Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo, alisema Tanzania na Poland zinajivunia ushirikiano mzuri walionao tangu wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka 1939-1945.Alisema wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, maelfu ya wananchi wa Poland walipewa hifadhi ya ukimbizi Tanzania Bara wakati huo ikijulikana kama Himaya ya Uingereza Tanganyika (Britain’s Tanganyika Territory).“Kulikuwa na kambi sita katika Tanganyika ambapo kambi kubwa ilikuwa kwenye Kijiji cha Tengeru mkoani Arusha na kambi zingine ndogo zilikuwa maeneo mbali mbali ikiwemo mkoani Kigoma, Kidugala na Ifunda (Iringa), Kondoa (Dodoma) pamoja na Morogoro,” alieleza Balozi Mwinyi.Kwa mujibu wa Balozi Mwinyi, wananchi hao wa Poland wakiwa nchini Tanzania, waliamua kujiendeleza kimaisha ikiwemo kujishughulisha na kilimo, biashara ndogondogo, kujenga kliniki, hospitali, makanisa na shule.Baada ya kwisha kwa vita hivyo, imeelezwa kuwa wengi wa wananchi hao wa Poland waliamua kurudi nchini mwao, lakini wengine waliamua kubaki Tengeru mpaka sasa. Kutokana na histori hiyo, Balozi Mwinyi alisema Poland imeendelea kuwa miongoni mwa washirika wakubwa wa Tanzania katika kukuza uchumi na kuboresha maisha ya watu.“Nchi zetu hizi mbili zinashirikiana kwenye kilimo, biashara, uwekezaji, elimu hususan kupitia udhamini wa masomo kwa Watanzania kusoma nchini Poland pamoja na sekta ya maji,” alieleza Balozi Mwinyi.Aliongeza kuwa Serikali ya Poland imesaidia katika uunganishwaji wa matrekta ya URSUS nchini kwenye Kiwanda cha TAMCO kilichopo Kibaha mkoani Pwani. Alisema Poland pia inatoa mafunzo kwa vijana wa Kitanzania namna ya kuunganisha na kutengeneza matrekta hayo.Mbali na mradi huo wa matrekta, alisema Serikali ya Poland pia inasaidia katika ujenzi na ukarabati wa maghala ya kuhifadhia nafaka kwenye mikoa minane ya Rukwa, Katavi, Manyara, Ruvuma, Dodoma, Shinyanga, Njombe na Songwe.Alisema maghala hayo yatakapokamilika, yataongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani za ujazo 251,000 za sasa hadi kufikia tani za ujazo 501,000. Kwa mujibu wa Balozi Mwinyi, Tanzania imeendelea kuvutia watalii kutoka Poland kwa kuwa kila mwaka watalii 12,000 hufika Kisiwani Zanzibar. Alisema idadi hiyo imeongezeka maradufu katika kipindi cha miaka miwili kwa kuwa mwaka 2016 watalii waliofika Kisiwani humo kutoka Poland walikuwa 7,000 tu.Kwa kuwa malengo ya Tanzania ni kufikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025, alisema ni muhimu kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi na kutoa wito kwa kampuni za Poland kuja kuwekeza nchini.Kwa upande wake, Balozi wa Poland nchini, Krzysztof Buzalski alisema anafurahi kuona ushirikiano wao na Tanzania unazidi kuimarika wakati ambao taifa lao linatimiza miaka 100 ya uhuru wake.Balozi Buzalski alisema Tanzania na Poland zinahitaji kushirikiana kwa dhati kwa kuwa ndiyo njia pekee ya nchi hizo kunufaika na fursa walizonazo kama vile teknolojia, bidhaa, kilimo na utalii.“Kama ulivyo msemo wa Kiswahili kwamba ‘Mvumilivu hula mbivu’, hivyo tunahitaji kuwekeza muda wetu, nguvu zetu na juhudi zetu ili tuweze kufanikisha haya,” alieleza Balozi Buzalski. | 3 |
HALMASHAURI za wilaya nane za mkoa wa Tabora, zimeanika fursa za kiuwekezaji zilizopo ndani ya wilaya hizo, kupitia jukwaa la biashara linaloendelea mkoani humo. Fursa hizo zimegusa maeneo mbalimbali ikiwemo ardhi ya kutosha ya uwekezaji katika kilimo cha mpunga, korosho kama zao la mkakati, tumbaku, alizeti, karanga na viazi vitamu, lakini pia ardhi kwa ajili ya viwanda vya kusindika asali na mazao ya mifugo.Halmashauri hizo nane za mkoa hio ni Nzega Mjini, Nzega, Urambo, Kaliua, Igunga, Sikonge, Manispaa ya Tabora na Tabora (Uyui). Akizungumza katika jukwaa hilo, lililoanza mjini Tabora jana, Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Angelina Kwinga, alisema katika wilaya hiyo imejaa fursa lukuki za kiuwekezaji ikiwemo ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi na uanzishaji wa viwanda mbalimbali vya kusindika mazao ya kilimo.Alisema pia wilaya hiyo inaongoza kwa kuzalisha asali bora kuliko inayozalishwa kwingine, inalima kwa wingi tumbaku, mpunga, alizeti na karanga. Aidha, alisema kutokana na zao la tumbaku kuwa moja ya chanzo kikubwa cha mapato katika wilaya hiyo, tayari wameanza mchakato wa kujenga kiwanda cha tumbaku, ambacho Rais John Magufuli ameahidi kutoa asilimia 70 ya fedha za gharama na halmashauri hiyo itatoa asilimia 0.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Peres Magiri alibainisha kuwa halmashauri hiyo ina fursa nyingi za uwekezaji kutokana na kuwa na rasilimali nyingi ikiwemo ardhi ambazo bado hazijatumiwa ipasavyo. “Tuna misitu ya kutosha na ndio maana tunazalisha asali bora. Pamoja na ukweli huo, bado uzalishaji wa asali uko chini ikilinganishwa na fursa ya uzalishaji iliyopo.Tunazalisha tani 2,000 wakati uwezo ni kuzalisha tani 6,000 kwa mwaka. Tunakaribisha wawekezaji katika eneo hili,” alisema Magiri. Aidha, mwaka 2013 wilayani humo, yaligunduliwa madini ya dhahabu katika kata ya Kitunda, ambayo kwa mujibu wa wataalamu ni mengi na yanahitaji uwekezaji wa kisasa katika uchimbaji. “Kwa sasa tuna wachimbaji wadogo 3,000” alisema.Pia, alibainisha kuwa tayari wameanza kujiandaa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha asali na wametenga fedha za awali Sh milioni 50. Alisema wanahitaji viwanda vitano zaidi vya asali ili kusindika asali na kuiuza kiubora zaidi. Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Gift Msuya alitangaza fursa za halmashauri hiyo ni kufikika kwake vizuri kutokana na wilaya hiyo kuwa na matoleo yanayoiunganisha na wilaya zote za Tabora, lakini pia maeneo mengine kama vile Kahama na Shinyanga.Alitaja fursa zilizopo wilayani humo ambako wanalima asilimia 80 ya mpunga kuwa ni uanzishwaji wa viwanda vya asali, mazao kama vile tumbaku, mpunga, asali, ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi, soko la kisasa, uwekezaji katika usafiri wa umma na huduma za kijamii kama shule, hospitali na taasisi za fedha.Kwa pande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kaliua, Dk John Pima, alisema Kaliua ndio halmashauri inayoongoza kwa kuwa na maeneo makubwa ya uwekezaji ikiwemo misitu kwa ajili ya mazao ya misitu kama mbao, asali na mabonde ya mpunga.Mkuu wa Wilaya ya Igunga, John Mwaipopo, alisema Igunga ina fursa nyingi ikiwemo mifungo zaidi ya milioni moja na ng’ombe zaidi ya 400,000, lakini kwa bahati mbaya kutokana na ukosefu wa viwanda, ngozi katika wilaya hiyo hutupwa.Alisema kutokana na hali hiyo, Igunga imeanzisha mkakati wa kuanzisha maonesho ya mifugo wakilenga kutoa elimu ya matumizi ya ngozi. Mchumi wa Manispaa ya Tabora, Joseph Kashushura, alisema tayari halmashauri hiyo imeanzisha miradi 38 iliyoko katika utekelezaji, iliyogusa maeneo ya viwanda, majengo, majisafi na salama, afya na elimu, masoko ya kisasa na usafirishaji. Jukwaa hilo la nane, limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) kwa kushirikiana na mkoa wa Tabora. Jukwaa la saba lilifanyika Agosti, mwaka huu mkoani Geita. | 3 |
KATIKA msimu wa kuelekea Krismasi na Mwaka Mpya, wafanyabiashara wa nguo wamesema biashara hivi sasa zimesimama, kwa kuwa hali ya mzunguko wake sio nzuri.Aidha, kwa upande wa bidhaa katika soko la Kariakoo, Dar es Salaam, hali ya biashara kwa sasa ipo ya wastani, kwa kuwa bidhaa nyingi zimepanda bei kutokana na uchache wa mazao. Hali hiyo ilibainika siku za karibuni HabariLeo ilipotembela eneo la Kariakoo kujionea hali halisi ya mauzo.Mfanyabiashara wa nguo sokoni Kariakoo, Masoud Juma alisema katika kipindi hiki biashara ni mbaya tofauti na matarajio yao. “Biashara ni mbaya sana, haijawahi kutokea, hali ni tofauti sana na matarajio ya wafanyabiashara wengi hasa katika msimu kama huu wa sikukuu kubwa kama hii ya Krismasi,” alisema. Alisema sababu kubwa ni wateja wamepungua.Aliomba ni wataalamu wa uchumi tu, ndio wanaoweza kueleza vizuri kupungua kwa wateja. Makamu Mwenyekiti wa Machinga Tanzania, Steven Lusinde alisema ingawa Krismasi inakaribia, haionyeshi kama kuna sikukuu ya aina yoyote, tofauti na miaka ya nyuma.Alisema kumekuwa na changamoto nyingi kwenye biashara, hali iliyofanya biashara nyingine zifungwe. “Soko linavurugwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na polisi, hivyo hali ya soko haiwezi kuwa imara,” alidai Lusinde. Ofisa Mipango wa Shirika la Masoko Kariakoo, Henry Rwejuna alitaja mazao yaliyopanda bei kwa sasa ni nyanya ambapo boksi moja linauzwa kati ya Sh 40,000 hadi 45,000, tofauti na siku za nyuma lilipouzwa kwa Sh 25,000.“Karoti bei ipo juu kiroba cha kilo 50 kinauzwa Sh 40,000 na Sh 45,000, ambapo kabla ya hapo ilikuwa Sh 20,000 na 25,000. Pilipili hoho mfuko kilo 1000 Sh 70,000 hadi 90,000, awali ulikuwa Sh 50,000 hadi 55,000,” alisema.Alisema ndimu kiroba kilo 50 kinauzwa Sh 80,000, kabla ya hapo ilikuwa Sh 40,000 hadi 45,000. “Nafaka hazijabadilika, ila matunda yamekuwa mengi bei imeshuka, ndizi mbivu tenga Sh 15,000 na Sh 20,000 kabla liliuzwa Sh 25,000 hadi 30,000.Embesikukuu zinazokuja, bali ni msimu tu wa mavuno. Wakati wafanyabiashara wa nguo wakilalamikia TRA, imeelezwa kuwa kwa muda mrefu watu hao wamekuwa wakikwepa kulipa kodi, kwa visingizio vya mashine za kielektroniki (EFDs) wanazotakiwa kutumia kuwa ni mbovu, kutumia risiti feki na kukwepa kutoa risiti kwa wateja wanaofika na kununua bidhaa mbalimbali.dodo moja linauzwa kati ya Sh 500 hadi 700, kabla liliuzwa Sh 1000. Vitunguu maji gunia la kilo 100 linauzwa Sh 80,000, kabla liliuzwa Sh 60,000 hadi 65,000,” alisema. Alisisitiza kuwa kwa bidhaa hizo, hivi sasa hazijaendana na maandalizi ya | 3 |
Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Henry Arika amebainisha hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari hiyo ili kushuhudia tishari hizo.Alisema ununuzi wake umegharimu jumla ya Dola za Kimarekani milioni 10 na yanatarajiwa kuongeza tija na ufanisi utakaoiwezesha TPA kuwahudumia wateja wake kwa kasi kubwa zaidi tofauti na ilivyokuwa awali.“Kwa kuwa tishari moja lina uwezo wa kubeba tani 3,500 au makasha 198 ya futi 20 kwa mara moja, hatua hiyo ni dhahiri itatupunguzia gharama za uendeshaji ambazo ni mizunguko ya kwenda nangani, mteja atapunguziwa muda wa kusubiri kwa kuwaongezea tija maradufu”, alisema.Hata hivyo alisema pamoja na ununuzi wa tishari hizo, TPA kwa kushirikiana na serikali inaendelea na mpango wake wa ujenzi wa bandari mpya Mwambani ambayo itawezesha meli kutia nanga moja kwa moja.Bandari ya Tanga ndiyo ya pili kwa ukubwa nchini ukiacha ile ya Dar es Salaam, ina gati lenye urefu wa mita 381 na kina kifupi cha maji ambacho hulazimisha mzigo kuhudumiwa mara mbili nangani na gatini ambapo shughuli za kupakia na kushusha hufanyika kwa kutumia tishari pamoja na meli za kuvuta vyombo. | 5 |
NA JOHANES RESPICHIUS, UNAWEZA kumuogopa utakapomuona akifanya yake kwenye filamu kutokana na kuvaa uhalisia ipasavyo hasa anapoigiza kikatili. Lakini pia anaweza kuigiza sehemu za huzuni vizuri sana. Anaitwa Mariam Ismail, staa huyu wa filamu za Kitanzania, amefanya vema kwenye filamu nyingi zikiwemo ‘Mr Kadamanja’ akiwa ameshirikishwa na Steven Charles Almas na marehemu Adam Kuambiana na Danija ambayo amecheza kama mke wa Jacob Steophen ‘JB’. Tumemdondosha mkali huyu ili kufahamu mengi ambayo huenda ulikuwa huyafahamu kutoka kwake akiwa ndani na nje ya tasnia ya filamu. Fuatilia… MY STYLE: Nje ya sanaa, wewe ni mtu wa aina gani? MARIAM: Mimi napenda sana sana maendeleo na nina ndoto ya kufika mbali kimaisha. MY STYLE: Ratiba yako ya siku huwa unaipangilia vipi? MARIAM: Ni ya kawaida lakini mara nyingi huwa inapangwa na management yangu kwahiyo nikija kuanza siku yangu nakuwa najua shughuli ya kufanya na inanilazimu kuitimiza kama ilivyopanga… kifupi sina ratiba maalum. MY STYLE: Tofauti ya Marium wa kwenye runinga na wa nyumbani ni ipi? MARIAM: Tofauti ipo na ni kubwa sana kutokana na nikiwa nyumbani nakuwa kama dada wa kawaida lakini nikiwa kwenye kazi huwa nakuwa serious. MY STYLE: Najua hujaolewa bado, mwanaume wa kukuoa anatakiwa kuwa na sifa zipi? MARIAM: Awe mcha Mungu, mwenye upendo na anisikilize kama mke wake. MY STYLE: Unatumia gharama kiasi gani ukiingia salon kuanzia nywele mpaka kucha za miguu? MARIAM: Inategemea na aina ya nywele ninayotaka kuweka… mara nyingi huwa napenda kuwa natural, yaani kuwa na nywele zangu halisia, ila siku nikiweka nywele natumia si chini ya 400,000, kucha ni 70,000. MY STYLE: Mara ya kwanza kucheza scene ya kukiss ulipata ugumu gani? MARIAM: Kiukweli sikiwahi kuona ugumu wowote kwa sababu hiyo ni kazi yangu niliyoamua kufanya, hivyo lazima nikubiliane na kila linalokuja mbele yangu. MY STYLE: Inasemekana ni lazima utembee na director ndiyo upewe nafasi kubwa ya kucheza filamu. Hilo unalizungumziaje? MARIAM: Kwangu halijawahi kunitokea, ila nadhani wanaofanyiwa hivyo wanakuwa wamejilengesha wenyewe ili wapewe u-main character, nadhani hao wanahisi kutembea nao ndiyo watapewa kipaumbele kucheza filamu nyingi na kuwa staa. Namshukuru Mungu William Mtitu alinitoa kutokana na uwezo wangu wa kuigiza na sijawahi kupata kikwazo chochote kwenye kampuni yake. MY STYLE: Ni skendo au jambo gani limewahi kukupata na huwezi kulisahau? MARIAM: Sijawahi kupata skendo na wala sizitaki kwani naamini zinaweza kunishushia heshima yangu. Naamini ustaa bila skendo inawezekana. MY STYLE: Umewahi kuachwa au kuacha na mpenzi wako? Ilikuwaje? MARIAM: Yote yamewahi kunikuta, kuachwa na kuacha, kwenye mapenzi kuna mambo mengi sana ambayo siwezi kuhadithia, ndiyo maana nikaamua nikae bila bugdha ya mapenzi, najaribu kujiweka mbali sana na mapenzi. MY STYLE: Jambo gani hujawahi kulisema sehemu yoyote na unadhani inaweza kuwa wakati muafaka sasa wa kuwaambia mashabiki zako? MARIAM: Mimi asili yangu nusu Mnyarwanda na nusu Mnyamwezi, pia kabla ya kuanza sanaa mwaka 2008 nilikuwa ‘Sungusungu’ eneo la Mbagala. MY STYLE: Unatumia kilevi gani? MARIAM: Kutokana na shughuli ninazozifanya siwezi kutaja aina ya kilevi ninachotumia kwa sababu nitakuwa kama nakipigia promo hicho kinywaji. Lakini kifupi napenda sana Spirits na Gin. MY STYLE: Mwisho kabisa, una ushauri gani kwa mastaa wanaotumia madawa ya kulevya? MARIAM: Toka enzi za akina marehemu Amina Chifupa, alipiga kelele nyingi sana kuhusu madawa ya kulevya, wenye kusikia watasikia. Lakini watu wamekuwa wakiendelea kuziba masiko na kuthubutu kuendelea na matumizi ya madawa hayo. Mimi sidhani kama naweza kuwa na ushauri zaidi, ni wao kuusikiliza na kufanyia kazi kwa sababu kama ni ushauri walishapewa sana na watu mbalimbali. | 1 |
Na WAANDISHI WETU- DAR ES SALAAM SIKU moja baada ya Rais Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Felichesmi Mramba, wasomi na wanasiasa wameibuka na kuzungumzia suala hilo. Wadau hao kwa nyakati tofauti jana walitoa maoni yao, huku baadhi yao wakikosoa utaratibu uliotumika kutengua uteuzi wa Mramba na wengine wakisifu hatua ya Serikali kugomea uamuzi wa Mamlaka ya Nishati na Maji (Ewura) kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 8.5 wakati huu ambao Serikali inahubiri sera ya uchumi wa viwanda. Katika maoni hayo pia wameonyesha wasiwasi wao juu ya uimara wa Menejimenti ya Tanesco, Bodi na uhusiano wa taasisi za Serikali na wizara ambapo walishauri kuondolewa mikanganyiko katika mabadiliko ya kisera na kuimarisha mifumo ya kisasa ya utendaji kazi. Wachambuzi wengine waliiambia MTANZANIA kuwa sakata zima la kupanda kwa gharama za umeme na hatua zilizochukuliwa dhidi ya Mramba halijakaa sawasawa huku wengine wakisema suala hilo linahitaji mjadala wa kitaifa. Profesa Semboja Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haji Semboja alisema kutenguliwa kwa mkurugenzi huyo kunatia shaka kwamba hakukuwa na mawasiliano mazuri kati ya Wizara ya Nishati na Madini na taasisi yake mama (Tanesco). Alisema jambo linaloshangaza na kuacha maswali kwa wengi ni jinsi mchakato wa kupandisha bei hiyo ulivyofanywa kwa uwazi na kushirikisha wadau wa umeme ambao walipewa nafasi ya kutoa maoni yao lakini mwisho wizara ikazuia. “Wakati mchakato unaanza wadau walipewa nafasi ya kutoa maoni yao, yalikusanywa na kwenda kujadiliwa, sasa labda Tanesco watuambie kama Serikali haikukubali wazo hilo la kupandisha bei,” alisema. Alisema hakuna asiyefahamu matatizo yaliyopo ndani ya shirika hilo kwani si mara ya kwanza kumekuwa na haja ya kuomba kupandisha gharama za umeme ili liweze kujiendesha kwa sababu ya mzigo mkubwa walionao. “Tunajua serikali ya sasa imeweka malengo makubwa na madogo, imelenga kuipeleka nchi katika uchumi wa viwanda, hivyo umuhimu wa umeme wa uhakika na wa bei nafuu unahitajika ili wawekezaji waweze kumudu gharama za kuendesha viwanda. “Kwa hiyo katika hili naweza kusema huenda Rais Magufuli aliona anapotezewa malengo yake, wakati akihamasisha wawekezaji wazawa wa ndani na wa nje kumiliki viwanda” alisema Profesa Semboja. Profesa Mpangala Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO), Profesa Gaudence Mpangala alisema suala hilo limegawanyika katika pande mbili, uhalisia wa bei za umeme za Tanesco na mfumo mzima wa utawala. “Bei walizopendekeza Tanesco binafsi sikuzifurahia hata kidogo kwani zilikuwa zinakwenda kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi, naipongeza Serikali kwa hatua yake ya kuzikataa. “Lakini kwa upande wa kiutawala, naona kuna walakini, suala kama hilo angelimaliza waziri mwenye dhamana na Ewura kwa sababu wana mamlaka hayo kisheria lakini hatua ya Rais Dk. Magufuli kuingilia, kutimua na kuteua hapo hapo si sahihi,” alisema. Alisema ili kujenga uchumi mzuri wa nchi ni lazima kuwepo na ushirikishwaji ambapo mamlaka ya juu inazipa uwezo wa kufanya maamuzi mamlaka za chini. “Mamlaka za chini zinashindwa kutoa maamuzi ndipo zinalazimika kisheria kufuata ngazi za juu ili zitoe maamuzi, sasa kama Rais anatoa uamuzi yeye mwenyewe moja kwa moja, atafanya mangapi,” alihoji. Aliongeza. “Waziri na Ewura walikuwa na uwezo wa kulimaliza suala hilo na iwapo ingeshindikana ingefuatwa ngazi ya Waziri Mkuu. “Kama huko nako ingeshindikana ndipo wangeenda kwa Rais lakini si hivyo ilivyofanyika si jambo zuri kiutawala. Ni vema mamlaka za chini ziachwe zifanye kazi yake. Hali hii inatia wasiwasi kwamba huenda wengine wanaondolewa kwa haki na wengine si kwa haki. “Wapo watakaotimuliwa lakini kumbe hawana hatia, mamlaka za chini zikiachwa zifanye kazi yake ni rahisi kubaini na pengine adhabu anayostahili mtumishi husika si kubwa kama inavyotolewa wakati huo na au labda angestahili onyo tu,” alisema. Profesa Mpangala alisema ni kweli Tanesco hupanga bei kisheria na Ewura hujadili na bodi huamua kiwango baada ya kupitia maoni ya wadau. “Lakini baada ya kuafiki bei, Ewura walipaswa kumwambia waziri husika waliyokubaliana kama hawakumwambia basi Ewura waliteleza katika hilo,” alisema Profesa Mpangala. Dk Onesmo Mhadhiri Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Onesmo Kyauke alisema uamuzi huo umetolewa kisiasa. “Suala la bei ya umeme ni siasa uchwara. Kuna wakati wanasiasa wanakuwa kama watoto, wanasema bei ya umeme haitapanda ili tuone kuwa serikali inawatetea wananchi kitu ambacho si kweli,” alisema. Mtatiro Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro alisema Tanesco inajiendesha kwa hasara kubwa kutokana na madeni na mikataba mibovu iliyolizingira shirika hilo. Alisema Serikali haijawahi kuchukua hatua madhubuti za kuliimarisha shirika hilo ili liwe la mfano katika utendaji na uzalishaji wenye faida na tija kwa taifa. “Kwa hiyo Tanesco imekuwa ikitegemea wateja wake ili kujikwamua kwa kila kitu jambo linaloifanya kuwa mzigo kwa watumiaji wa umeme na wala si serikali. Kila uamuzi utakaofanywa na serikali juu ya Tanesco wanaoathirika na uamuzi huo ni wananchi,” alisema. Mtatiro alipongeza uamuzi uliofanywa na Waziri Profesa Muhongo wa kuzuia bei mpya za umeme zisianze kutumika kwani ongezeko hilo la asilimia 8.5 zilikuwa mzigo kwa wananchi wa kawaida na si serikali. “Kinachoshangaza zuio la waziri limekuja dakika za mwisho za utekelezaji wa jambo ambalo limefanywa kwa mchakato wa wazi na ambao umeshuhudiwa na kubarikiwa na serikali yenyewe. “Kuna mtu katumbuliwa, ametumbuliwa kosa lake nini? Je ni kufuata mchakato wa kisheria na kikanuni na kupandisha bei ya umeme? “Kama serikali ilikuwa na nia njema kwa nini haikuizuia Ewura na Tanesco mapema, zisiendelee na hatua za namna hiyo? Kwa nini wasubiriwe wafanye uamuzi wa kisheria ndipo Mkurugenzi wa Tanesco afukuzwe? Hivi kweli tatizo la Tanesco ni mtu au ni taasisi?,” alihoji Mtatiro. Zitto Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) alipinga ongezeko la gharama za umeme, uonevu na kuvunjwa sheria huku akihoji mamlaka ya Waziri wa Nishati juu ya Ewura. “Waziri kwenye tamko lake kataja sheria ya umeme ya mwaka 2008 ( nilishiriki kuitunga neno kwa neno wakati William Mganga Ngeleja ni Waziri na William Shelukindo mkt wa Kamati). Naomba kusaidiwa kifungu cha Sheria alichotumia Waziri. Kifungu mahususi na si jumla jumla tu,” alisema. Habari hii imeandaliwa na Christina Gauluhanga na Veronica Romwald- Dar es Salaam | 3 |
Na FESTO POLEA, JUNI 7, 1988 mwanadada, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ alizaliwa. Uwezo wake wa kipekee wa kufikiri tofauti na kufanya mambo kwa umahiri mkubwa ndiko kunakomweka tofauti na watu wengine katika kazi zake mbalimbali ikiwemo uandishi wa nyimbo, ujasiriamali, uigizaji, utangazaji wa runinga na redio pamoja na uimbaji. Mwanadada huyo mzaliwa wa Arusha aliyewahi kutangaza kwa mafanikio kwenye kituo maarufu cha runinga cha MTV, shindano la Bongo Star Search na kipindi cha Dume Condom kwa sasa anatamba na wimbo wa ‘Cash Madame’ uliozua maswali mengi kama ni jibu la wimbo alioshirikishwa wa ‘Dume Suruali’ wa msanii Khamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ aliyezaliwa mwaka 1984. Kwanini ni jibu? Nyimbo hizi mbili zinahisiwa kuwa ni jibu kutokana na ujumbe wake ambapo ‘Dume Suruali’ unamzogoa mwanamke mpenda fedha huku ‘Cash Madame’ ukimpa ujasiri mwanamke apende zaidi fedha. Baadhi ya maneno ya Mwana Fa katika wimbo wa ‘Dume Suruali’ ni ‘Nihonge nanunua nini kwanini yani kuna kipi nisichokijua ina tv ndani…’, ‘usipende ela kama mfuko au fanya ufanyavyo upate zako…’, ‘Na ujifunze pesa zinauza utu wako…’, ‘Unapenda ela zangu nami nazipenda pia kila mtu abaki na zake…’, ‘Na ukiniomba kesho unisikii tena kwani unauza nini dada…’. Vanessa naye anaanza kwa kuimba ‘Dharau na pesa mi sitaki, eti mimi dada wa ku-party nasikia nina wengi mashuga dady, sipigi kazi niwie radhi’ Vanessa kuhusu Cash Madame, Dume Suruali “Hapana si jibu la ‘Dume Suruali’ wimbo wa ‘Cash Madame’ niliurekodi Desemba mwaka jana na nimeutoa Desemba mwaka huu lakini huu wa ‘Dume Suruali’ nilioshirikishwa na Mwana FA tuliurekodi Agosti mwaka huu, ni mawazo tu yamegongana kutokana na ujumbe wake mmoja kuelezea wanawake mwingine kuelezea wanaume,” anafafanua Vanessa. Vanessa anaongeza kwamba wimbo wa ‘Dume Suruali’ ulipotoka uliwaumiza baadhi ya wanawake walioona kama wanasemwa vibaya na wanaume kutokana na ujumbe uliopo katika wimbo huo hivyo alipotoa wimbo wake wa ‘Cash Madame’ wanawake wengi waliufurahia wakiona kama amewajibia. Kisa cha Cash Madame? Vanessa anaeleza kwamba kisa cha kuandika wimbo huo kinatokana na kudhulumiwa kwake na mmoja wa mwaprodyuza wenye majina makubwa Afrika. “Kuna prodyuza mkubwa Afrika Mashariki alinidhulumu fedha zangu, kisa kilikuwa hivi, tulikubaliana anilipe kiasi fulani cha fedha lakini akawa anasumbua wakati mimi nikiwa nimeshafika ukumbini, mashabiki wengi wa Afrika Mashariki walihudhuria, nilifikiria mengi niliona ningegoma ningewakera na kuwapoteza mashabiki wangu wengi, niliamua kupanda jukwaani niliamini angenilipa baada ya shoo lakini haikuwa hivyo, alinidhulumu hapo ndipo nilipopata wazo la kuandika wimbo huu nikipinga dhuluma kwa wasanii hasa wa kike,” anaeleza Vanessa. Anasema wimbo huo aliuandika kwa ajili ya wanawake wote wapiganaji akiwatia moyo waendelee kupigana katika kusaka haki zao na wasikubali kudhulumiwa licha ya vikwazo mbalimbali wanavyokutana navyo huku wakiamini kwamba Mungu ni wetu wote. “Nimewatia moyo sana ndiyo maana mstari wa kwanza wa wimbo huo nimesema: ‘Dharau za pesa mi sitaki…,’’ anaeleza. Wanenguaji wake Kuhusiana na wanenguaji wake anasema huwa anaishi nao kama ndugu, aliwashauri wasiache kazi wanayoifanya ndiyo maana kwa sasa wapo nchini Marekani kwa kazi hiyo hiyo ya unenguaji inayowaingizia fedha nyingi za kujikimu na maisha yao. “Wale ni ndugu zangu, naishi nao kama wadogo zangu, baada ya kumaliza upigaji picha za video yangu ya ‘Cash Madame’ jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini chini ya mwongozaji Justin Campos, wamekwenda Marekani kwa kazi yao itakayokamilika Januari mwakani ndiyo watarejea nchini,” anaeleza Vanessa. Aliingiaje kwenye muziki? Mwaka 2012, Vanessa alijiunga na studio ya B’Hits wakatoa wimbo alioshirikishwa na msanii mwenye mafanikio makubwa nadni na nje ya Afrika, Ambwene Yessayah, aliyezaliwa Julai 5, 1981 huko mkoani Mtwara. Baadaye akashirikishwa pia na msanii Ommy Dimpoz katika wimbo wa ‘Me and You’ ambao aliutendea vyema na ukamwonyesha njia ya mafanikio katika uimbaji ikiwemo wimbo wa ‘Siri’, ‘Hawajui’, ‘Closer’ hadi hivi sasa. Vitu alivyoshiriki Vanessa ameshiriki vitu vingi vikiwemo kampeni ya kupinga malaria. Mwaka 2008, akiwa balozi wa Alive Foundation alitembelea Uwanja wa fisi akiwa na balozi mwenzake, Kelly Rowland. Mwaka 2009, alikuwa mtangazaji Tamasha la Sauti za Busara International Music Festival na mwaka 2011 alikuwa mtangazaji wa kituo cha redio kijulikanacho kama Choice Fm ambapo aliwahi kufanya mahojiano na wasanii mbalimbali akiwemo, Kelly Rowland, Mac Miller, Rick Ross, Ludacris na wengine wengi. | 1 |
['Manchester United inajiandaa kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, kwa Real Madrid au Juventus mwezi huu, lakini wanataka £150m. (Express)', 'Manchester United inapania kuwanunua viungo wa kati wa Aston Villa Jack Grealish, 24, na James Maddison, 23, kutoka Leicester. (Independent)', 'Wachezaji wengine wanolengwa na United ni kiungo wa kati wa Juventus na Ujerumani Emre Can, 25, na Sean Longstaff, 22, wa Newcastle. (ESPN)', 'Aston Villa ina mpango wa kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Michy Batshuayi, 26, kwa lengo la kumpatia mkataba wa kudmu. (Footmercato - in French)', 'Villa pia wanamtaka mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Olivier Giroud, 33. (Sun)', 'Mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 30, ameelezea kujitolea kwake kwa Arsenal na kutuliza tetesi za kuondoka kwake mwezi Januari. (Evening Standard)', "Arsenal imeingia katika kinyang'anyiro cha kumsaka beki wa Bournemouth na Uholanzi Nathan Ake, 24. (Telegraph)", 'Inter Milan ni moja ya klabu zilizowasiliana na wawakilishi wa kiungo wa kati wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen. Kandarasi ya kiungo huyo wa miaka 27 inakamilika msimu huu wa joto. (Sky Sports)', 'Manchester City inatarajiwa kurefusha kwa mwaka mmoja mkataba wa kiungo wa kati wa Brazil Fernandinho, 34. (Sun)', 'Dau la Chelsea la yuro milioni 40 la kumnunua mshambuliaji wa Ufaransa Moussa Dembele ,23, limekataliwa na Lyon. (Footmercato - Kwa Kifaransa)', 'Aston Villa inatafakari uwezekano wa kuweka dau la kumnunua kipa wa Stoke City Muingereza, Jack Butland, 26. (Mail)', 'Ajax imesitisha mpango wa kumnunua beki ya Tottenham na Ubelgiji Jan Vertonghen kwa sababu bei ya mchezaji huyo wa miaka 32 ni ghali sana . (De Telegraaf - Ujerumani)', 'Southampton wanataka kumsaini beki wa Valladolid raia wa Ghana Mohammed Salisu, 20. (Sky Sports)', "Leicester imeipiku Arsenal katika kinyang'anyiro cha usajili wa beki wa Juventus na Italia, Daniele Rugani, 25. (Express)", 'Arsenal imemuulizia winga wa Atletico Madrid na Ufaransa Thomas Lemar, 24. (Marca - ya Uhispania)', 'Real Madrid imewasiliana na wawakilishi wa mshambuliaji wa Liverpool na Senegal Sadio Mane, 27. (Le10Sport)', 'Manchester United na Tottenham wanatarajiwa kukabiliwa kwa ushindani mkali wa kumnunua kiungo wa kati wa Lille Mfaransa Boubakary Soumare,20, huku ofa sita za kumnunua zikiripotiwa kupokelewa na klabu yake. (Mail)'] | 4 |
Na LEONARD MANG’OHA- DAR ES SALAAM MIEZI 12 ya mwaka 2016, ilikuwa ni ya aina yake hasa baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kutangaza operesheni ya Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) ambayo ilikuwa inakwenda sambamba na maandamano nchi nzima. Operesheni hiyo ilitangazwa kufanyika Septemba Mosi, ambapo pamoja na mambo mengine ilikuwa iambatane na kufanyika kwa mikutano na maandamano nchi nzima. Hatua hiyo ilizua taharuki kwa Serikali pamoja na wananchi huku vyombo vya dola likiwemo Jeshi la Polisi likilazimika kuandaa askari wake na magari maalumu yaliyokuwa yakiranda mitaani yameandikwa ‘Vunja Ukuta’. Mbali na hilo pia askari hao walikuwa wakifanya mazoezi katika miji mbalimbali nchini ikiwa ni ishara ya kujiandaa na wafuasi wa Chadema watakaokuwa wamejitokeza kwa lengo la kufanya maandamano mitaani. Akitangaza maazimio ya kikao cha Kamati Kuu Julai 27, mwaka huu, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema hatua hiyo imechukuliwa ili kujenga jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani. “Ni wazi sasa kuwa, kuna tishio kubwa dhidi ya ukuaji wa demokrasia hapa nchini mwetu kutoka kwa viongozi wa serikali hii ya awamu ya tano ambao wanakandamiza demokrasia na madhara yameshaanza kulitafuna taifa letu,” amesema Mbowe. Alitaja baadhi ya matukio ya ukandamizaji wa haki na demokrasia nchini kuwa ni kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaendelea kufanya mikutano. Jingine ni kupiga marufuku urushwaji wa moja kwa moja wa matangazo ya Bunge na kudhibiti wabunge wa upinzani bungeni kupitia Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson. Matokeo mengine ni kuingilia mhimili wa mahakama, kupuuza utawala wa sheria, serikali kupeleka mswada kandamizi wa Sheria ya Haki ya Kupata Habari, serikali za mitaa kunyang’anywa mapato na serikali kuu na uteuzi wa wakurungezi, makatibu tawala wa wilaya bila kuzingatia sheria ya utumishi wa umma. “Mbali na hayo, serikali pia imetoa maelekezo kupitia mawasiliano yake na mabalozi kuelekeza kuwa, kabala ya mabalozi au maofisa wa ubalozi kukutana na asasi zisizo za kiserikali au vyama vya siasa ni lazima kwanza waombe kibali cha serikali kupitia wizara ya mambo ya nje. Pamoja na mambo mengine, chama hicho kilisema lengo la operesheni hiyo ni kuzuia matukio ya ukandamizaji wa haki na demokrasia nchini, kiliyodai kuwa yanafanywa na Rais Dk. John Magufuli. Akizungumzia chimbuko la Ukuta, Mbowe alisema umetokana na Rais Magufuli kupiga marufuku safari zote za nje kwa watumishi wa umma, kuamuru Mahakama Kuu iwahukumu wafanyabiashara ambao wana kesi za kodi ili Serikali ishinde. Mbowe alitaja sababu nyingine kuwa ni Serikali kuendeshwa kwa matamko badala ya Katiba na sheria, Serikali kuwafukuza na kuwadhalilisha wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na mikutano ya kisiasa kupigwa marufuku. Polisi waonya Agosti 23 Jeshi la Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam kupitia kwa Kamishina Simon Sirro lilipiga marufuku maandamano hayo na kusema hakuna mtu atakayethubutu kuingia barabarani kutokana na jeshi la polisi kujipanga kuhakikisha wananchi wanafanya shughuli zao bila kuingiliwa na kitu chochote. Baada ya marufuku hiyo ya Polisi ilifuatiwa na viongozi wa kiserikali wakiwemo wakuu wa mikoa, wilaya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ambao wote walipinga operesheni hiyo na kusema kuwa ina nia ovu ya kuleta machafuko nchini. Kutokana na vuguvugu hilo Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam lilifanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiashara mmoja, Yoram Mbyelllah, mkazi wa Mburahati Dar es Salaam kwa tuhuma za kuuza fulana zenye maneno ya uchocezi. Mbowe ahojiwa Katika hatua nyingine Agosti Mosi mwaka huu Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisisitiza kuwa licha ya viongozi wa chama hicho kutishwa msimamo wao kuhusu operesheni Ukuta uko pale pale. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam baada ya kuhojiwa na kuachiwa kwa dhamana Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Lissu alisema msimamo wao uko palepale na hakuna kilichobadilika. “Wamemuhoji kwa taarifa aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari juu ya msimamo wa chama wa kufanya mkutano nchi nzima. Tatizo jeshi letu wakisikia maandamano, mkutano au mtu anamsema Magufuli basi anatuhumiwa kwa uchochezi. “Wametumia muda mrefu kumuhoji lakini mwisho wamemwachia kwa dhamana na amewahi ‘Airport’ ili aende kuhudhuria mazishi ya kamanda wetu Senga (Joseph) na watamwita watakapomhitaji tena,” alisema Lissu. Ukuta waahirishwa
Septemba 30 ikiwa zimebaki mbili kabla ya kufanyika kwa operesheni hiyo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alitangaza kutofanyika kwa Operesheni Ukuta pasi kutaja tarehe ya kufanyika operesheni hiyo kwa kile alichodai ni kutompa adui nafasi ya kujipanga. Awali operesheni hio ilikuwa ifanyike Septemba Mosi mwaka huu lakini iliahirishwa kutoa nafasi kwa viongozi wa dini kukutana na kujadiliana na Rais Dk. John Magufuli juu ya mustakabali wa hali ya kisiasa nchini. | 3 |
WAZIRI wa Kilimo, Japhet Hasunga amesema namna ambavyo Rais John Magufuli anavyoongea na kutenda ni sawa Mwasisi wa Taifa la Tanzania, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.Hasunga aliyasema hayo juzi alipotembelea eneo la Ihumwa ambako ujenzi wa ofisi mpya za Wizara ya Kilimo zimeanza jijini Dodoma. Alisema Baba wa Taifa ndiye aliyetoa wazo la Dodoma kuwa Makao ya Chama Tawala pamoja na Serikali, lakini kwa miaka kadhaa wazo hilo lilikuwa halijawahi kutekelezwa, lakini Rais Magufuli analitekeleza kwa vitendo.Aliongeza kuwa baada ya utekelezaji wa wazo hilo la kuhamia Dodoma kwa serikali, Rais Magufuli aliagiza wizara zote zijenge ofisi katika eneo moja na kwa kulitekeleza jambo hilo, wizara zilipewa mgawo maalumu wa fedha kwa ajili ya kujenga ofisi za kudumu katika eneo la Ihumwa. “Napenda nimpongeze Mheshimiwa Rais wetu kwa kulisimamia wazo hili la kuwa na eneo maalumu na rasmi la kuwa ofisi kwa wizara zote na moja kati ya faida ni kuwa wananchi ambao wamekuwa wakisafiri kutoka mikoa mbalimbali kwa ajili ya kupata huduma katika ofisi za umma, sasa watapata unafuu wa kuhudumiwa katika eneo moja kama hapa, ambapo kila wizara itapatikana,” alisema Hasunga.Alisema jambo hilo ni sawa na utekelezaji wa Oparesheni Sogeza ambapo Baba wa Taifa alianzisha mwaka 1974 ili kuhakikisha wananchi wanakaa pamoja ili serikali iwahudumie kwa haraka zaidi na kwa ufanisi zaidi. “Wazo la Mhe. Rais John Pombe Magufuli kuhamia Dodoma na Ofisi za Serikali kukaa pamoja hivi, jambo hili linafanana na wazo la Baba wa Taifa kupitia Oparesheni Sogeza ambapo wananchi wanawekwa pamoja ili serikali iwajibike sawasawa kwa wananchi,” alisema.Waziri huyo alifanya ziara ya kushtukiza kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi za Wizara ya Kilimo ambako kwa kuanzia wizara inajenga ofisi za wakuu wa idara na vitengo na baadaye zitajengwa ofisi za watumishi wengine katika eneo hilo la pamoja. Akizungumza kuhusu kukamilika kwa ujenzi huo, alisema mkandarasi alipewa lengo la kukamilisha Desemba 31, 2018, lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake, kazi hiyo inatarajia kukamilika Februari 12, 2019.Naye Fundi Mkuu wa majengo ya Wizara ya Kilimo, Meja Onesmo Njau alisema kama ambavyo mpango kazi wao unavyoonesha kazi kuanza rasmi Desemba 10, 2018, na wanataraji kukamilisha na kukabidhi rasmi Februari 12, 2019 na kuongeza kuwa taasisi yao ya Suma JKT imepewa jukumu muhimu na la heshima na watamaliza kwa wakati. | 3 |
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam juzi na Naibu Gavana wa BoT, Juma Reli wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya PBZ na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, wateja pamoja na waumini wa dini mbalimbali.Alisema Benki Kuu ndiyo yenye jukumu la kusimamia mifumo ya uendeshaji wa kibenki kwa benki zote zilizopo nchini na kwamba katika kuhakikisha benki za Kiislamu zinafanya kazi zake kulingana na misingi iliyojiwekea ni vyema utaratibu huo ukawepo.“Inatambuliwa wazi kuwa benki hizi zina utaratibu wa utoaji wa huduma kwa kuzingatia masuala ya riba, BoT imeona vyema kuwa na kanuni maalumu zitazoziwezesha benki hizo kufanya kazi zake kwa utaratibu unaoeleweka ili kuziondolea usumbufu,” alisema.Alisema katika kuhakikisha hilo linatekelezeka tayari mchakato wa uandaaji wa kanuni hizo umeshaanza kufanyiwa kazi na wakati wowote utakapokuwa umekamilika utaingizwa katika utaratibu kwa ajili ya utekelezaji.Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya PBZ mmoja wa viongozi wa benki hiyo Said Said alisema benki hiyo yenye idadi ya matawi manne Tanzania Bara na Zanzibar inazidi kujiimarisha kadri siku zinavyokwenda na hivyo kuwapa imani ya kuwa na nguvu zaidi miaka ijayo. | 5 |
JUMLA ya Tuzo 62 zitatolewa kwa viongozi, taasisi, idara, balozi, sekta za umma na binafsi zinazofanya vizuri ikiwemo ya Heshima kwa Marais wawili Rais John Magufuli na Rais wa China, Xi Jinping. Tuzo ya Heshima itatolewa kwa marais hao wawili kutokana na jitihada na mchango wao wa kipekee uliotukuka katika kulinda, kutetea, kuendeleza, kuchochea na kusimamia raslimali na kuleta maendeleo endelevu ya jamii zao. Akizungumza jijini hapa jana, Mwenyekiti wa Tuzo za Jamii Tanzania (Tanzania Awards International Limited), Deonatus Malegesi alisema tuzo hizo zitakazotolewa Aprili 13, mwakani zinatolewa kwa mara ya pili na mara ya kwanza zilitolewa mwaka 2015 ambapo tuzo ya heshima alipewa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Malegesi alisema mchakato wa kutafuta washindi una baraka zote za Ikulu na utafanyika kwa ushirikiano katika kutafuta washindi kwa njia ya upigaji kura na utafiti na utazinduliwa Oktoba 14, 2019 na kilele chake kitakuwa Aprili 13, 2020 ambapo tuzo zitatolewa na mgeni rasmi, Rais John Magufuli. Malegesi alisema pia itatolewa tuzo kwa mbunge bora, mwanasiasa mwenye mafanikio katika siasa za Tanzania, kampuni bora ya michezo ya kubahatisha na timu bora ya mpira wa miguu miongoni mwa Yanga, Simba na Azam. | 3 |
WATU watatu wamekufa na wawili wamejeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, baada ya kufukiwa na kifusi kwenye machimbo ya moramu.Machimbo hayo yanayotumika kwa ajili ya shughuli za ujenzi, yapo eneo la Moivaro katika Kata ya Moshono jijini hapa.Tukio hilo limetokea umbali wa kilometa nane kutoka katikati ya Jiji la Arusha, baada ya mabonge makubwa ya moramu kuporomoka, wakati watu hao wakiwa kwenye shughuli ya uchimbaji.Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Jonathan Shana alisema tukio hilo ni la Aprili 23, mwaka huu saa 2:00 asubuhi.Kamanda Shana alisema tangu kutokea ajali hiyo vikosi vya uokoaji kutoka mamlaka za ulinzi na usalama, vilikusanyika eneo la tukio na kuendelea kufukua udongo, kuwatafuta watu waliofukiwa. “Lakini pia vifaa mbalimbali vya uokoaji viliwasili mara moja ili kufanikisha ufukuaji kifusi linaenda kwa haraka na vizuri,” alisema Kamanda Shana.Alisema watu watatu waliofariki, walikuwa wamefunikwa na ngema iliyobomoka kutokana na mvua zilizonyesha usiku wa kuamkia siku hiyo na wawili walijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini. Alishukuru Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), mgambo, viongozi mbali mbali na jeshi lake kwa kufanya kazi hiyo kuwa rahisi. Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqarro alisema hiyo ni mara ya pili kwa machimbo hayo kuporomoka na kusababisha maafa.Kwamba mwaka 2013 hali kama hiyo ilijitokeza na kuua watu 13 na wengine kadhaa kujeruhiwa. “Lakini katika tukio hili watu watatu waliofariki baada ya kufukiwa na gema lililobomoka kutokana na mvua zilizonyesha usiku wa jana na wawili walijeruhiwa na gema tu na tumewakimbiza hospitalini,” alisema. Shuhuda wa ajali hiyo, Ruben Jacob ambaye ni mchimbaji wa moramu Moivaro, alisema aliona gari linapakia moramu chini ya machimbo hayo, ila ghafla alisikia kishindo kikubwa cha kuanguka kwa gema na kufunika watu.“Viongozi mbali mbali walipofika niliona miili mitatu imetolewa chini ya kifusi na watu wawili walikimbizwa hospitalini kwa matibabu,” alisema Jacob. Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Calist Lazaro alisema taarifa ya kufukiwa kwa watu hao, aliipata asubuhi na alijaribu kusambaza taarifa kwa viongozi wenzake, ambao walitoa mashine za kuchimba kifusi ili kuokoa watu hao. “Wizara ya Madini kama imetoa leseni ya uchimbaji sisi jiji tutachukua ushuru, ila sina hakika sababu machimbo haya yalifungiwa, lakini nitafuatilia baada ya shughuli hizi kuisha,” alisema. | 3 |
Nchemba aliyasema hayo mwishoni mwa wiki bungeni mjini hapa wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge zilizotolewa katika mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2015/16.Akijibu hoja hizo, ambazo nyingi zilitolewa na wabunge wa vyama vya upinzani wakisema serikali haijafanya chochote katika miradi ya maendeleo bali kilichoongezeka ni deni ya taifa, Nchemba alisema hata kama TRA na Halmashauri zote nchini zingekusanya mapato kwa asilimia 100, zingefikia asilimia 62 ya bajeti.“Kwanza watu wanaotazama bunge hili huko nje wakiwasikia hawa wanaosema serikali haijafanya chochote watawashangaa, wengi wanalalamika deni la taifa limeongezeka, ila miradi ya maendeleo iliyofanywa hawaioni…”,alisema Nchemba.Alifafanua, ikiwa TRA pekee ingekusanya mapato kwa asilimia 100 fedha hizo zingekuwa ni asilimia 57 ya bajeti na kwamba kama rais angeamua asikope taifa lingekuwa wapi hivi leo, hakuna nchi iliyotulazimisha kukopa,ila hiyo asilimia inayobaki ya bajeti ni lazima ipatikane kwa wahisani,” alisema Nchemba.Na kuwashangaa wabunge wa upinzani ambao wamekuwa wakibeza miradi mbalimbali na kusema kama wanapenda miradi iliyofanywa ni lazima wapende na deni lililopo.“Hivi unalipendaji jengo la bunge tunalokaa humu ndani ambalo tumelijenga kwa mkopo halafu usiupende mkopo wenyewe, utakipendaje Chuo Kikuu cha UDOM, kilichojengwa kwa mkopo alafu usipende deni lake”, hivyo hivyo kwa miradi ya barabara, umapita kwenye barabara nzuri halafu hampendi madeni yake,” alihoji Nchemba.Na kusema miradi ipatayo 360 iliyotekelezwa nchini imekamilika na mingine iko kwenye hatua za mwisho kutokana na fedha za mikopo kutoka kwa wahisani wa maendeleo, na kwamba hata reli ambayo inagharimu Sh trilioni 15 ni fedha za mkopo.“Ni vyema tukatimiza wajibu wetu, na ni heri aliyechoka kwa kufanya kazi kuliko yule mvivu aliyechoka kwa kutotambua kazi zilizofanywa,” alisisitiza Nchemba.Na kusema deni la nchi lililofikia takribani Trilioni 30, Nchemba alisema bado linalipika kwani kuna viashiria vyote vinavyoonesha ulipikaji wake na kwamba nchi haiwezi kuendelea bila kuwa na mikopo.“Tumekopa nchi mbalimbali, India, China, Japan na nchi nyingine na fedha zimetumika kwenye miradi ya maendeleo na leo mmeona mafanikio yake , kuna mtandao wa barabara za lami ambao umerahisisha usafiri kwa wananchi na kuokoa muda. | 5 |
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka wazazi nchini kulinda usalama wa watoto wao dhidi ya vitendo vya ubakaji na ulawiti kwa kutoruhusu ndugu au jamaa kulala chumba kimoja na watoto hao pindi wanapokwenda kuwatembelea.Ameziagiza halmashauri zote kuanzisha mabaraza ya watoto ili kuwapa fursa ya kujadiliana masuala mbalimbali yanayowahusu, hatua ambayo pia itawasadia katika kuwajengea uwezo wa kujieleza na kujiamini mbele ya jamii inayowazunguka.Waziri Mwalimu ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam juzi kwenye maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya haki za watoto, yaliyohudhuriwa na viongozi wa kitaifa na kimataifa akiwemo Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.Alisema pamoja na mapambano dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea kufanywa nchini, bado wapo baadhi ya watu wamekuwa wakifanya vitendo hivyo dhidi ya watoto huku mengi ya matukio hayo yakihusisha ndugu wa karibu wa familia hizo, suala alilodai kuwa kuna haja ya jamii kubadili fikra.“Ni vyema sasa tukageukia watu wetu wa karibu, imefika mahali hata ndugu yako akija nyumbani usikubali kumruhusu alale chumba kimoja na mtoto wako ni bora ukalala naye mwenyewe kwa lengo la kulinda usalama wake, kwani matukio mengi ya ulawiti na ubakaji siku hizi yanayonyesha ndugu ndiyo wahusika ,” amesema.Katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa pia na wanafunzi mbalimbali kutoka shule za msingi, sekondari na vyuo, Waziri Mwalimu pia aliwataka wazazi kuacha kuwakalipia watoto pale wanapokosea na badala yake washirikiane nao katika mambo mbalimbali yanayowahusu, hatua aliyodai kuwa itawasaidia kutimiza ndoto zao za kimaisha.Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, Maniza Zaman, alisema katika kuadhimisha siku ya watoto duniani, jamii zinapaswa kuwa karibu na watoto na kuachana na vitendo vya ukatili dhidi yao kwa lengo la kulinda kizazi kijacho.Alisema katika kuhakikisha kuwa haki za mtoto zinalindwa, Unicef imekuwa ikitoa elimu mbalimbali kwa lengo la kuondoa fikra hasi na kujenga fikra chanya katika jamii kwa lengo la kulinda ustawi wa watoto hao duniani kote. | 3 |
JUMATANO ya wiki hii Ligi Kuu soka Tanzania Bara ilianza rasmi, ambapo kulishuhudiwa baadhi ya timu zikishindwa kutamba katika viwanja mbalimbali,huku wababe Simba,Yanga na Azam FC wakipata ushindi katika michezo yao ya kwanza ya ufunguzi. Mashabiki wa soka wengi walikuwa wakisubiri kwa hamu urejeo wa Ligi hiyo ili kuona uhondo wa timu zao pamoja na kuona ufundi wa miongoni mwa wachezaji wapya waliosajiliwa katika timu hizo.Ikiwa katika Uwanja wa Taifa dhidi ya Tanzania Prison, Simba ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 lililofungwa na Mnyarwanda Meddie Kagere na kuifanya Simba kuibuka na pointi tatu katika mchezo wa ufunguzi. Haikua siku nzuri kwa Tanzania Prisons iliyoweka kambi visiwani Zanzibar, kwani pamoja na kupambana ilijikuta ikipoteza mchezo wake wa kwanza. Katika Uwanja wa Mabatini, Ruvu Shooting iliangukia pua kwa kupoteza bao 1-0 dhidi ya Ndanda FC, wakati Wagosi wa Kaya, Coastal Union iliyopanda daraja iliambulia sare dhidi ya Lipuli FC ya Iringa.Singida United pamoja na usajili mzuri walioufanya ilishindwa kutamba mbele ya timu iliyopanda daraja ya Biashara kutoka mkoani Mara, baada ya kufungwa kwa bao 1-0 na kuanza kwa kupoteza, Mbao ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Alliance, wakati Kagera Sugar walianza vyema baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Mwadui ya Shinyanga. Ligi hiyo iliendelea juzi Alhamisi kwa michezo minne ,JKT Tanzania ikiwa nyumbani ililazimishwa sare na vijana wa Ettiene Ndayiragije timu ya KMC ya Kinondoni, wakati Stand ilitumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuifunga African Lyon bao 1-0.Michezo ya wababe wawili iliyopigwa usiku,Yanga ilikuwa Uwanja wa Taifa kukipiga dhidi ya Mtibwa mchezo uliokuwa na ufundi mkubwa kutokana na ubora wa kila timu, hata hivyo, Mtibwa ilishindwa kutamba na kuambulia kichapo cha mabao 2-1, sifa na pongezi nyingi zilienda kwa mshambuliaji Heritier Makambo aliyefunga bao la kwanza na kuonesha uwezo mzuri pia.Mchezo mwingine ni Azam FC ikiwa Chamazi dhidi ya Mbeya City na kushuhudiwa wakiifunga timu hiyo kutoka Mbeya kwa mabao 2-0 na kuanza Ligi kwa kupoteza. Ni Biashara Mara pekee iliyoweza kuibuka na ushindi miongoni mwa timu zilizopanda daraja wengine wakiambulia sare na kupoteza. Pia wachezaji wapya waliosajiliwa katika kila timu ndiyo wameonekana kuzibabe zaidi klabu kongwe za Simba na Yanga,ingawaje zimeshindwa kuibuka na ushindi wa mabao mengi katika michezo hiyo. | 4 |
SERIKALI ya Tanzania imekubaliana na serikali ya Sudan Kusini kuimarisha ushirikiano katika sekta ya usafirishaji ili nchi hiyo ipitishe mizigo kwenye bandari ya Dar es Salaam.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amewaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa, ushirikiano kati ya nchi hizo ulikuwepo tangu mwaka 2011 lakini sasa unaimarika zaidi.“Itakumbukwa kwamba uhusiano kati ya Sudan Kusini na Tanzania ulianza tangu mwaka 2011 walipopata uhuru lakini sasa uhusiano huu unaimarika katika usafirishaji kwa kutumia bandari,”amesema Waziri Kabudi.Amesema Februari mwaka huu serikali za nchi hizo zilikubaliana kushirikiana kielimu na kwamba, Tanzania imekubali kuisaidia Sudan Kusini kutengeneza vitabu vya Kiswahili, kuendelea kutoa mafunzo ya lugha hiyo, na kuwapa walimu wa kufundisha shule za msingi na sekondari.Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Uganda, lengo la serikali ni kujenga bomba la mafuta kwenda Sudan Kusini ili kuifungulia nchi hiyo milango ya kibiashara."Kwa mwaka wanasafirisha tani 700,000 hadi 800,000 lakini sasa uhusiano huu unaimarika vizuri, hii ni kutokana na utendaji kazi kwa serikali hii ya awamu ya tano," amesema Kamwelwe.“Sudan Kusini wameona waje Kusini mkataba ili mizigo yao yote ipite Dar es Salam, sasa tunaendelea na ukarabati wa usafiri wa reli na wa anga, jengo la tatu la abiria (TB III) Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) tumekabidhiwa kwa hiyo wafanyabiashara hawatapata taabu kuja kukagua mizigo yao ," amesema.Waziri wa Viwanda, Biashara na Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Sudan Kusini, Paul Mayom Akech amesema Tanzania ina historia kubwa na Sudan Kusini hivyo wataimarisha mkataba huo ili Tanzania iendelee kuwasaidia.“Tumeonesha nia yetu ya kushirikiana na Tanzania na tuko tayari, tunaamini huu unaweza kuwa mwanzo mzuri kwetu kibiashara kwa sababu tuna fursa nyingi, tunaamini mtaendelea kutusaidia kama ambavyo mmekua mkitusaidia" amesema.Waziri huyo pia ameiomba Tanzania kuingilia kati kusuluhisha uhusiano kati ya Khartoum na Juba kibiashara kwa kuwa si mzuri. | 5 |
BAADA ya ukimya wa muda mrefu kwa mchezaji Ibrahimu Ajibu kurejea kwenye kikosi cha Simba akitokea kwa mahasimu wao Yanga, amevunja ukimya na kudai amendoka kwa amani bila kinyongo na mtu yeyote.Alisema amefanya hivyo kwa kujua wazi kazi yake ni kucheza mpira kuna leo na kesho mambo yakiharibika iwe rahisi kwake kurudi tena kwa miamba hao waliomfanya ang’are vilivyo msimu uliopita.Nyota huyo kwenye msimu ulipita wa Ligi Kuu Tanzania Bara alitoa mchango mkubwa kwenye kikosi cha Yanga , mbapo alisaidia mara 17 na kupachika mabao saba kiasi cha kumfanya aliyekuwa mshambuliaji Heritier Makambo kufunga mabao mengi.Ajibu amesema amejiandaa vizuri kukabiliana na upinzani wa kupigania namba kwenye kikosi hicho kuhakikisha anawakonga nyoyo mashabiki wa timu hiyo wanaonekana kufurahishwa na ujio wake huo baada ya kuwa nje ya kikosi hicho kwa miaka miwili.“Nimejiandaa vizuri kulinda kiwango changu na kuhakikisha natengeneza nafasi na kutoa pasi za mwisho kama nilizokuwa natoa nikiwa Yanga, Nawaomba mashabiki wa Simba wasiwe na wasiwasi mambo mazuri yanakuja, “amesema Ajibu. | 4 |
CHUO Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha St Joseph, kimeandaa maonesho maalumu ya ubunifu kwa wanafunzi wanaosoma katika chuo hicho.Chuo hicho kimeahidi kuendelea kutoa wataalamu wa kutosha watakaosaidia kusukuma ajenda ya Tanzania ya Uchumi wa kati wa viwanda.Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Burton Mwamila amesema jijini Dar es Salaam kuwa, maonesho hayo yanatarajiwa kufanyika Agosti 29 hadi 31 Mlimani City, Dar es Salaam, kwa lengo la kutoa msukumo kwa jamii na hasa wanafunzi kupenda masomo ya sayansi.Amesema kupitia maonesho hayo yaliyopewa jina la ‘STEM’ mbali na madhumuni yake ya kuonesha vipaji, wanafunzi wanaosoma chuoni hapo, pia yatatoa fursa kwa wananchi watakaoyatembelea kupima afya na kuchangia damu.“Huu ni utaratibu wetu wa kuonesha vipaji walivyonavyo wanafunzi wetu katika kubuni mambo mbalimbali yanayoweza kuleta tija kwa jamii, wataalamu na kampuni zinazoamini katika ubunifu zinaweza kujitokeza na kuona namna watakavyoweza kuendeleza ubunifu wa vijana hawa,” alisema Profesa Mwamila.Aidha alisema katika kukuza vipaji vya wanafunzi wanaosoma katika chuo hicho pamoja na kusukuma ajenda ya Tanzania ya uchumi wa kati wa viwanda ifikapo Mwaka 2025, chuo hicho kimejikita kwa kutoa elimu ya nadharia kwa wanafunzi wake, kwa lengo la kuwapa ujuzi wa kutosha.Katika hatua nyingine, Profesa Mwamila alipongeza ushirikiano uliopo baina ya waandisi nchini, huku akiwataka kuzidisha ushirikiano huo kwa hatua zaidi zitakazowawezesha kupata kazi katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli.Amesema kuelekea maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Bodi ya waandisi nchini(ERB), waandisi wa Tanzania wamefanya kazi nyingi zinazotambulika na hata kuliletea heshima taifa na kwamba kinachotakiwa kwa sasa ni kuzidisha umoja baina yao ili waweze kufanya mambo mengi zaidi. | 3 |
NAIROBI, KENYA RAIS wa zamani wa Kenya, Daniel arap Moi,
amefikishwa hospitalini kufanyiwa ukaguzi wa afya yake kwa mara ya pili katika
muda wa wiki mbili. Vyombo vya habari vya Kenya vimeripoti kuwa msemaji
wa kiongozi huyo, Lee Njiru, alisema yupo hospitali anahudumiwa na kikosi cha
wataalamu wa afya wanaoongozwa na daktari wake, David Silverstein. “Yupo macho (Moi) na anafahamu
kinachoendelea,” alisema Njiru. Awali gazeti la Daily Nation kwa kunukuu duru kutoka
familia ya kiongozi huyo, lilisema Moi alikimbizwa hospitalini Jumapili baada
ya kupata matatizo ya kupumua. Hata hivyo, Daily Nation linaripoti kuwa jamaa
mwingine kutoka familia ya Moi alikanusha taarifa hiyo. Familia hiyo imeeleza katika taarifa yake kutofurahishwa
na habari ambazo imezitaja kuwa ‘mbaya na za kuzusha mshtuko’ zinazosambazwa. Gazeti jingine nchini humo la The Star,
limeripoti kwamba Moi yuko katika hali mahututi. Si mara ya
kwanza taarifa za kiongozi huyo wa zamani kuugua kusambaa katika vyombo vya
habari nchini. Mwishoni
mwa mwaka jana palikuwa na taarifa pia za Moi kufikishwa hospitalini kufanyiwa
uchunguzi kama ilivyo kwa wakati huu. Kwa mara
nyingine, Njiru alinukuliwa na vyombo vya habari akisema; “Mzee
aliruhusiwa kwenda nyumbani baada ya matabibu wakiongozwa na daktari wake
Silverstein kuridhika na afya yake baada ya uchunguzi.” Kwa mujibu
wa taarifa kutoka ofisi yake iliyotumwa kwa vyombo tofauti vya habari, Machi
mwaka jana kiongozi huyo mstaafu alipelekwa Hospitali ya Ichilov huko Tel Aviv,
nchini Israel ambako taarifa zilieleza alikwenda kufanyiwa uchunguzi. Baada ya
kulazwa kwa muda aliruhusiwa kurudi nchini Kenya ambako ilibainika baadaye
kwamba alikwenda kufanyiwa uchunguzi wa goti lake lililokuwa linamsumbua. Raila Odinga ni miongoni mwa viongozi
wa kisiasa waliofika Kabarak, ambako ndio anakoishi Moi, ili
kumtakia afya njema baada ya kulazwa hospitalini nchini Israel kwa takriban
mwezi mmoja. Moi alizaliwa Septemba mwaka 1924 katika eneo la
milimani huko Baringo eneo la Bonde la Ufa kaskazini mwa Kenya. Aliinukia kutoka kuwa kijana aliyekuwa mchungaji
mifugo na kuwa mwalimu katika shule ya kimisionari na baadaye kushikilia
usukani wa taifa kama rais wa pili Kenya alipomrithi Jomo Kenyatta. Chini ya utawala wa Kenyatta, alikuwa makamu wake
wa rais. Alipokea wadhifa wa rais Agosti mwaka 1978 baada ya Kenyatta kufariki
dunia. Aliiongoza Kenya kwa miaka 24 kuanzia mwaka 1978
hadi 2002. Moi alikuwa kiongozi pia wa chama tawala wakati
huo cha Kanu, kilichofanikiwa kupata ushindi katika uchaguzi miaka kadhaa
nchini Kenya. Kanu kilipoteza ushindi mwaka 2002, wakati Mwai
Kibaki akiwa na muungano wa kisiasa wa National Rainbow Coalition
alipochaguliwa kuwa rais wa Kenya. | 2 |
Na BENJAMIN MASESE
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amemtahadharisha Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, John Wanga, kwamba endapo atashindwa kusimamia vema agizo la urasimishaji makazi holela na uandaaji wa hati miliki kwa wananchi, atatumbuliwa.
Alitoa tahadhari hiyo juzi baada ya kusomewa taarifa ya utekelezaji wa urasimishaji na uandaaji wa hati za ardhi ambako Halmashauri ya Ilemela imetekeleza kwa asilimia moja kwa kuandaa hati 834 huku viwanja vingine 16,000 vikiwa vimepimwa bila kuandaliwa hati.
Lukuvi ambaye alionekana kukasirishwa na hali hiyo alisema kushindwa kuandaliwa hati hizo ndani ya Halmashauri ya Ilemela ambayo ina maofisa ardhi na watathmini zaidi ya 40 kmeisababishia hasara Serikali.
Alisema kazi hiyo ingefanyika ilivyotarajiwa serikali ingepata mapato ya Sh bilioni 2.5 kwa mwaka lakini kilichopatikana ni Sh bilioni 1.3 tu.
“Hakuna halmashauri nchini iliyo na watumishi wengi wa idara ya ardhi kama Ilemela na Nyamagana mara zote nimekuwa nikifikiria kuwahamishia wilaya nyingine kama Geita kwa Mheshimiwa Rais, Dk. John Magufuli ambako hakuna hata mmoja.
“Lakini leo pamoja na wingi wenu mnaandaa hati 834 huku viwanja 16,000 mkishindwa kuvikamilisha kwa muda niliotoa.
“Sasa Mkurugenzi nakuambia kwamba Serikali imewavumilia vya kutosha na sasa kama hautabadilika kwa muda ambao nimekuongezea kuanzia sasa hadi Juni 30, mwaka huu tambua kwamba kitambi chako kitapata pancha.
“Wewe mwenyewe utajua namna ya kuiziba pancha hiyo, hatuwezi kuimba wimbo huo huo kila mwaka.
“Kuna viti vitu vidogo vidogo vya hapa halmashauri mnavifinyia kazi lakini suala ambalo ni la muhimu mnashindwa kukamilisha.
“Nilikuwa namuona mkurugenzi ni mjanja lakini anachokifanya hapa ni kama kutwanga maji kwenye kinu kwa sababu kodi ya ardhi haikusanywi,” alisema.
Waziri alisema Halmashauri za Ilemela na Nyamagana zinatakiwa zikamilishe hatua hiyo Juni 30, mwaka huu atakapoifunga rasmi na kutangaza ‘masterplan’ ya Jiji la Mwanza ifikapo Agosti.
Aliwataka wananchi kutambua kuwa baada ya kufungwa urasimishaji makazi haitatokea tena fursa ya namna hiyo.
Alisema wananchi ambao hawatakuwa na hati ya eneo analoishi watahesabika kama wavamizi, hivyo watapoteza haki yao na maeneo hayo yatachukuliwa na Serikali kwa shughuli nyingine.
Lukuvi alisema Serikali kuu imetenga Sh bilioni 22 kwa ajili ya masterplan ya Mwanza ambayo itaanza kutekelezwa Agosti mwaka huu, kazi ambayo itafanywa na wataalamu kutoka China. | 3 |
Kwa ushindi huo, Mlandizi Queens imefikisha jumla ya pointi 15, ambazo zimeshindwa kufikiwa na timu zingine tano zilizoshiriki hatua hiyo ya sita bora iliyotoa bingwa.Nyota wa mchezo huo alikuwa mwanadada Mwanahamizi Omary ambaye peke yake alipachika wavuni mabao manne na kufanikiwa kuondoka na mpira baada ya kufunga `hat trick’ pamoja na bao moja zaidi.Mwanahamisi ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia Mlandizi Queens bao katika sekunde ya 45 na kuwa bao la mapema zaidi kufungwa katika ligi hiyo ya wanawake nchini.Bao la pili lilifungwa na Fadhila Yusuph katika dakika ya 11 baada ya kuwazidi mbio mabeki wa Panama kabla Mwanahamisi ajafunga la tatu katika dakika ya 35 akichia shuti kali lililomshinda kipa Edina Ndelwa.Hadi timu hizo zinakwenda mapumziko, washindi walikuwa mbele kwa mabao 3-0.Mwanahamisi alifunga bao la nne na tano katika dakikaya 65 na 76 na kukamilisha idadi ya mabao manne katika mchezo mmoja na kuiwezesha timu yake kutwaa taji hilo.Katika mchezo uliotangulia asubuhi, timu ya Marsh Queens iliifunga Fair Play kwa mabao 3-0. | 4 |
BAADA ya Hospitali ya Benjamin Mkapa kufanya kwa mafanikio upandikizaji wa fi go kwa wagonjwa wanne, kuanzia sasa huduma hiyo itakuwa ikitolewa hospitalini hapo na wataalamu wa ndani.Hatua ya kuwapandikiza figo wagonjwa wanne, sasa inafanya kufikia wagonjwa 11 ambao wamepatiwa huduma hiyo tangu kuanza kutolewa kwake. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini hapa baada ya kupandikizwa wagonjwa wengine wanne, Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk Alphonce Chandika alisema baada ya upandikizaji huo wa watu wanne, itakuwa ni mwisho kuja kwa jopo kubwa la wataalamu kutoka Japan, kushiriki katika utoaji wa huduma hiyo kutokana na madaktari wa wazawa kukomaa.“Kuanzia Januari 6 mwaka huu tulianza upandikizaji wa figo na tumepandikiza kwa watu wanne na umefanyika kwa umakini na tumepata mafanikio makubwa,”alisema na kuongeza: “Tuna madaktari wanne ambao wamepata mafunzo kuhusu upandikizaji figo, hawa wameenda Japan mara mbili sio kwenda kuangalia bali kushiriki kwenye upasuaji na upandikizaji maana kule wenzetu wanafanya mara kwa mara,”alisema.Aidha, Dk Chandika alisema tangu kuanza huduma ya upandikizaji figo katika Hospitali ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM) pamoja na wataalam kutoka Tokushukay Medical Corporation nchini Japan, wagonjwa 11 wamepatiwa huduma hiyo huku mamilioni ya fedha yakiokolewa.Akifafanua, Dk Chandika alisema kwa kawaida upandikizaji figo kwa mgonjwa mmoja, unagharimu kati ya Sh milioni 22 hadi Sh milioni 25. Kwamba gharama ya matibabu hayo kwa nje ya nchi ni zaidi ya Sh milioni 100.Alisema gharama inayotumika kwa mgonjwa mmoja nje ya nchi, inaweza kuhudumia wagonjwa watano katika Hospitali ya Benjamin Mkapa. Kwamba kwa wagonjwa saba wa awali, kiasi cha Sh milioni 700 kiliokolewa.Mwenyekiti wa jopo la wataalam kutoka Japan, Profesa Kobayashi Shuzo alipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuimarisha huduma za kibingwa, ikiwemo za upandikizaji figo na kwamba hospitali hiyo mbali na kutoa huduma kwa watanzania wataweza kuhudumia pia wanaotoka mataifa mengine. | 3 |
NAIROBI, KENYA
VINARA wa muungano wa upinzani wa Nasa kutoka jamii ya Waluhya wametangaza vita ya kisiasa dhidi ya Kiongozi wa chama cha ODM, Raila Odinga na kuwataka wafuasi wao kukikataa chama hicho kuelekea uchaguzi wa mwaka 2022. Wakihutubia mikutano ya hadhara katika vituo kadhaa vya biashara katika Kaunti ya Vihiga, Kiongozi wa chama cha Ford Kenya, Moses Wetang’ula na mwenzake wa ANC, Musalia Mudavadi, walisema Odinga ameikosea heshima jamii ya Waluhya kwa kuisaliti na kuitelekeza. Walitaja hatua ya kuondolewa kwa Wetang’ula kutoka uongozi wa wachache katika seneti na wao kudaiwa waoga kuwa ishara tosha ODM ‘imeidharau’ jamii ya Waluhya. “Mliona namna alivyotukwepa na kwenda kuzungumza na Rais Uhuru Kenyatta. Na juzi mliona alivyochochea kuondolewa ofisini kwa ndugu yangu Wetang’ula kama kiongozi wa wachache katika seneti.”
“Huyo ni msaliti na sisi kama jamii ya Waluhya tukiepuke kabisa na chama chake kinachoshirikiana na Jubilee,” Mudavadi aliwaambia wafuasi wake mjini Mbale bila kumtaja Odinga kwa jina. Nao viongozi wa ODM wakiongozwa na Katibu Mkuu Edwin Sifuna na Mbunge wa Ugunja, Opiyo Wandayi, waliwajibu kwa kupuuzilia mbali malalamiko yao. “Watu wanapaswa kuungana kwa masuala yenye umuhimu kwa wananchi kama vita dhidi ya umasikini unaowazonga watu wetu. Si masuala potofu kama kuwashambulia wanasiasa wengine,” alisema Sifuna.
Naye Wandayi alisema: “Hakuna aliyeisaliti jamii ya Waluhya. Hakuna mwanasiasa aliye na uwezo kama huo. Hili suala la mabadiliko ya uongozi katika seneti linashughulikiwa na maseneta wenyewe, haifa kutumiwa kumchafulia jina kinara wetu Odinga”. Migawanyiko imeibuka ndani ya NASA baada ya Odinga kukutana na Rais Uhuru Kenyatta kwa mazungumzo Machi 9 bila kuwahusisha vinara wenzake. | 2 |
KULWA MZEE –dar es salaam MFANYABIASHARA Waziri Mizoge, aliyekutwa na dawa
za kulevya gramu 2193.1 nyumba ya kulala wageni Tunduma, amehukumiwa kwenda
jela miaka 40 na kulipa faini zaidi ya Sh milioni 200. Mizoge alihukumiwa juzi na Mahakama Kuu Mkoani
Songwe mbele ya Jaji Dk. Adam Mambi, baada ya mahakama kuridhishwa na ushahidi
wa Jamhuri kwamba alifanya makosa hayo. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Achiles Mulisa
alidai mshtakiwa alikamatwa Mei 4 mwaka 2012 katika nyumba ya kulala wageni
inayoitwa Nice Shirez, Tunduma akiwa na heroine gramu 1645.89 na mchanganyiko
wa heroine na cocaine gramu 547.21. Baada Jamhuri kuthibitisha mashtaka bila kuacha
shaka, mahakama ilimtia hatiani na kumuhukumu kwa makosa yote mawili. Katika kosa la kwanza la kukutwa na gramu 1645.89,
mshtakiwa alipewa adhabu ya kwenda jela miaka 20 na kulipa faini ya Sh
73,873,350. Kosa la pili la kukutwa na mchanganyiko wa
heroine na cocaine, amehukumiwa kwenda jela miaka 20 na kulipa faini ya Sh
197,080,450. Mshtakiwa alikutwa na gramu 2193.1 za dawa za
kulevya na anatakiwa kwenda jela miaka 40 na kulipa faini ya Sh 270,953,800 kwa
makosa yote. Mahakama imeamuru dawa ziteketezwe. Wakati huo huo, Mwinyi Rajabu Mkazi wa Magomeni
na Ally Hamad Mkazi wa Mbezi Luis, Dar es Salaam wamehukumiwa kwenda jela kwa
kosa la kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroine kilo 63.155. Washtakiwa hao walihukumiwa na Mahakama Kuu
Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, mbele ya Jaji Lilian Mashaka. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Saraji Ebora
akisaidiana na Wakili wa Serikali, Kauli Makasi, walidai kwa nyakati tofauti kuwa
washtakiwa walikamatwa Novemba 7 mwaka juzi maeneo ya mpaka wa Kalambo mkoani
Mtwara. Washtakiwa walikamatwa wakiwa wameficha dawa hizo
katika gari aina ya Toyota Alphard yenye namba za usajili T 499 DCI. Mahakama iliwatia hatiani baada ya kuona mashtaka
dhidi yao yamethibitishwa bila kuacha shaka. Washtakiwa wamehukumiwa kwenda jela miaka 20 na
mahakama imeamuru gari lililotumika kusafirisha dawa hizo litaifishwe na kuwa
mali ya Serikali. | 3 |
Na MAULI MUYENJWA, DAR ES SALAAM RAIS mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki, amewakumbusha wasomi kuhusu malengo mazito ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ya kuanzisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Akizungumza wakati wa mahafali ya 46 ya UDSM baada ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari na Rais mstaafu Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mkuu wa chuo hicho, Mbeki alisema lengo kubwa ilikuwa ni kuzalisha wasomi ili kutatua matatizo yaliyopo katika jamii. Mbeki alisema lengo la Mwalimu Nyerere ambalo alilitoa mwaka 1963, la kuwa na elimu ya juu iliyojikita kuwapata wataalamu katika nyanja mbalimbali, ambao wangeweza kufanya tafiti na kuyapatia majibu matatizo yaliyopo katika jamii, bado halijatimia. “Kuna changamoto nyingi kama mabadiliko ya hali ya hewa, kutojua ni namna gani ya kutumia rasilimali za asili, vita, migogoro ya mipaka na mengineyo, lakini yote haya yalitakiwa kutatuliwa na wasomi na ndilo lilikuwa lengo kubwa la kuanzishwa elimu ya juu Afrika,” alisema Mbeki. Aliwataka wanafunzi wanaohitimu katika fani mbalimbali kutumia elimu zao katika kutatua matatizo yaliyopo katika jamii na kuacha kukumbatia vyeti na kukaa navyo bila faida yoyote. Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, alitumia fursa hiyo kuaga kuhudhuria kama Makamu Mkuu wa Chuo kwa kuwa muda wake umefikia ukingoni. “Miaka 10 iliyopita nimekuwa nikihudhuria sherehe hizi tangu mwaka 2006, sherehe hizi ni za mwisho, muda wangu umefikia ukingoni na siku chache zijazo nitakabidhiwa mrithi wa nafasi hii atakayeteuliwa,” alisema Profesa Mukandala. Alitoa rai kwa wanafunzi waliohitimu kuwa anaamini wameandaliwa vizuri, hivyo jamii inawategemea katika kuleta maendeleo kwa nchi na hata dunia nzima. Mwanzo wa mahafali hayo rais mstaafu wa awamu ya nne, Kikwete, alisimikwa rasmi kuwa mkuu wa chuo hicho ambapo kuanzia jana ataanza majukumu yake kama Mkuu wa a UDSM. Profesa Mukandala alisema mwaka huu kutakuwa na jumla ya wahitimu 6,717, ambapo kati yao, 61 watatunukiwa shahada ya uzamivu, 627 shahada za umahiri na 59 stashahada ya uzamili na jumla ya wahitimu 5,968 watatunukiwa shahada za awali. | 3 |
Bakari Kimwanga na Gabriel Mushi, DODOMA NAIBU Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amesema wabunge wanawake wamesikitishwa na kushindwa kwa mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Chama cha Democrat, Hillary Clinton. Dk. Tulia alitoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma jana, baada ya kutambulisha wageni mbalimbali. Alisema walitarajia mambo yangekuwa mazuri upande wao akiwa mama (wanawake), lakini haikuwezekana. “Safari hii haikuwezekana, asikate tamaa maana baada ya miaka minne mambo yanaweza kuwa mazuri zaidi kuliko ilivyokuwa sasa. Nampa pole mama Clinton kwa kuwa safari hii haikuwezakana,” alisema Dk Tulia huku akishangiliwa na wabunge wanawake na kuongeza: “Nasikia kuna watu hapa wanasema tungempeleka mheshimiwa fulani… katika maeneo yale mama Clinton angeshinda,” alisema. Kutokana na kile kilichoonekana kupigwa butwaa na uchaguzi huo, kabla ya kuuliza swali la nyongeza jana asubuhi, Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (Chadema), alisema ana masikitiko makubwa kwa sababu Hillary Clinton ameshindwa uchaguzi. “Kwa niaba ya wanawake wenzangu, nampa pole mama Clinton kwa kushindwa uchaguzi, tumeumia sana na tumerudi nyuma,” alisema. Kauli hiyo ilimfanya Dk. Tulia kumtaka aeleze amepata wapi taarifa wakati bado wabunge wanawake wana faraja Hillary angeweza kushinda. Hata hivyo, akijibu swali la Suzan, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Khamis Kigwangala, alimpa pole Hillary kwa kushindwa kwenye uchaguzi huo. | 3 |
Rais John Magufuli amefuta katazo la matumizi ya wimbo wa taifa, bendera na nembo lililotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.Hivi karibuni wizara hiyo iliandika barua yenye kumbukumbu namba CHA.56/193/02/16 ya Novemba 23, 2018 ikiwa ni baada ya kupokea maelezo kutokea Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi.Barua hiyo ilienda kwa Wakuu wa Vyuo vya Ualimu, Wa Maendeleo ya Jamii, Wakuu wa Vyuo Vikuu, Vyuo Vikuuu Vishiriki pamoja na Taasis zilizopo chini ya Wizara hiyo. Agizo hilo limekuwa likikosolewa na watu mbalimbali ambao wamepinga uamuzi huo huku wengine wakitumia mitandao ya kijamii kukosoa uamuzi huo.Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Ikulu, ilimnukuu Rais Magufuli akisema kuwa agizo la wizara limetoa maelezo ambayo yanaathiri uzalendo wa watanzania. Pia alisema, linatoa mkanganyiko wa tafsiri ya rangi na alama zilizopo kwenye bendera ya Taifa.Alisema,“hata mimi mwenyewe tangia ninasoma ninafahamu kuwa rangi ya njano kwenye bendera inawakilisha madini na ni madini ya aina zote, na sio dhahabu peke yake kama inavyosema barua hiyo ya wizara. “Kutokana na utata huo basi, ninafuta maagizo kwenye barua hiyo na kama kuna tatizo ni lazima utaratibu uzingatiwe kwa kuwa hilo ni jambo la kitafa na sio mtu mmoja”. Rais aliagiza pia kuwa bendera, nembo na wimbo wa taifa viendelee kutumiwa kama ilivyokuwa awali kabla ya kutolewa kwa agizo hilo. | 3 |
WAKALA wa Huduma za Misitu nchini (TFS) imeunda timu ya utafi ti wa wataalamu wakiwemo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo(SUA), kuchunguza kwa kina ugonjwa unaoshambulia na kunyausha miti ya kupandwa mkoani Rukwa na kuwasababishia hasara kubwa wenye mashamba ya miti.Ofisa Mtendaji Mkuu wa TFS, Profesa Silayo Dos Santos alibainisha hayo juzi wakati akizungumza na gazeti hili. Alithibitisha kuwa bado ugonjwa huo unaoshambulia miti iliyopandwa mkoani humo, haujajulikana.“TFS tumeshaunda timu ya utafiti ya wataalamu kutoka TFS, TAFORI (Tanzania Forestry Research Institute), Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) na Tropical Forestry Research Institute(TIPRI) kufanya uchunguzi kwa haraka iwezekanavyo “alieleza.Hata hivyo, hakueleza ni lini wataalamu hao watawasili mkoani Rukwa, kufanya utafiti wao ili kubaini ugonjwa unaonyausha miti hiyo, iliyopandwa na kutafutia ufumbuzi wa changamoto hiyo.Awali Jaji mstaafu Peter Chocha ambaye pia ni mwanaharakati wa mazingira, alieleza hofu yake ya hatari ya Mkoa wa Rukwa kugeuka kuwa jangwa, kutokana na miti mingi iliyopandwa mkoani humo kushambuliwa na ugonjwa, am- bao bado haujajulikana kitaalamu na kusababisha miti kunyauka na kufa.Alieleza hayo, alipokuwa akichangia katika katika kikao cha kupitia na kuboresha kazi wa utunzaji wa mazingira mkoani Rukwa, kilichoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la mazingira la Rukwa Environmental Management Society (REMSO).Kwa mujibu wa Mratibu na Mfuatiliaji wa Shirika lisilo la kiserikali la Wanasheria,Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo ( LEAT),Grace Shio alilieleza gazeti hili kuwa kikao hicho kilichofunguliwa na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa, Bernard Makali kimeratibiwa na kudhaminiwa na mradi wa Jumuiko la Pamoja, Suluhisho la Pamoja(JUPASUPA) kupitia LEAT.“Kila mahali miti iliyopandwa yenye umri wa miaka sita imenyaushwa baada ya kushambuliwa na ugonjwa ambao kitaalamu bado haujajulikana, nimetembelea vijiji vingi vikiwemo Msanzi, Mtai , Mwimbi na Ulinji athari ni kubwa sana. Nimeshawasiliana na Mtendaji Mkuu wa TFS (Profesa Dos Santos ) nikamweleza changamoto hii ambayo inatishia mkoa wa Rukwa kuwa jangwa, pia imewasababishia wenye mashamba ya miti hasara,”alisisitiza . | 3 |
Na MARTIN MAZUGWA, WAHENGA walisema ukicheka na nyani utavuna mabua, ni msemo kama misemo mingine iliyowahi kusemwa, lakini ikiwa na maana kubwa kama itaweza kufafanuliwa kwa umakini na kutambua maana halisi ya kile inachomaanisha. Hakuna nyumba isiyo na msingi na kama ipo na ajitokeze mjenzi wa nyumba hiyo ajisifu kwa ubunifu wake, ninachoamini mimi msingi na ubora wa kitu unatokana na maandalizi yake ya awali ambayo ndiyo hutoa taswira halisi ya kitu. Msingi wa Ligi Kuu unatokana na Ligi Daraja la Kwanza, kwani timu ili ipande ni lazima ipitie ligi hiyo ndipo ipande daraja, timu zinazoshiriki Ligi Kuu zimetoka huku chini na kuweza kufika hapo zilipo, ligi ya awali imeonyesha kusahauliwa kutokana na mambo ambayo yamekuwa yakifanyika katika viwanja mbalimbali. Kilio kikubwa kwa timu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ni suala la ukata na kukosekana kwa wadhamini, kitu kinachopelekea wachezaji kukosa mishahara pamoja na posho. Timu nyingi zinazoshiriki ligi hii, zinategemea viingilio vya mashabiki wanaoingia uwanjani kwa ajili ya kuendesha baadhi ya mambo, ikiwemo kutoa mishahara pamoja na kufanya usajili wa wachezaji wao na benchi la ufundi. Kitendo cha kupata mapato kidogo ya viingilio vya uwanjani, yanasababishwa na baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya mchezo wa soka hapa nchini, ikiwemo wafanyabiashara wa soko la Machinga Complex ambalo ni kikwazo kikubwa katika Uwanja wa Karume. Madhara ya haya ni makubwa, kwani ni sababu ya kutofanya vizuri kwa baadhi ya timu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, hivi sasa mpira unahitaji gharama kubwa ili uweze kufanya vizuri. Huwa siamini kama kweli Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limeshindwa kabisa kuwazuia wale wote wanaokaa katika jengo la biashara la Machinga Complex, kwani wamekuwa wakiangalia mpira pasipokuwa na hofu ya aina yoyote ile na wasimamizi wa Ligi wakiwa kimya kana kwamba suala hili hawalioni. Jambo hili ambalo ni zito limekuwa halipewi uzito unaostahili, kwani ikiwa suala hili halitachukuliwa hatua mapema litakuwa na athari kubwa kwa soka la nchi hii hapo baadaye. Taratibu jambo hili limeanza kukua, watu wengi wamekuwa wakikaa juu ya jengo hilo huku mashabiki wachache na wapenda soka wakiingia uwanjani na kuzisapoti timu zao pindi zinapocheza. Kama hali itaendelea kuwa hivi kila siku, haitokuwa ajabu kusikia baadhi ya timu zikishindwa kusafiri, kwani watu wengi wamekuwa wakiangalia michezo mingi pasipo kutoa hata senti tano, jambo linaloziumiza baadhi ya timu ambazo hazina udhamini na zinajiendesha zenyewe kwa kutegemea michango ya mashabiki na wanachama. Ili kuweza kudhibiti suala hili, ulinzi unapaswa kuimarishwa katika soko hili, pindi michezo ya Ligi Daraja la Kwanza inapochezwa ili kuweza kudhibiti uhalifu huu ambao umeanza kukua kwa kasi kubwa, huku wimbi kubwa la watu ambao wanakaa katika soko hilo kuangalia mpira likiongezeka. Mazoea hujenga tabia, imekuwa ni kama wafanyabiashara hawa wamepewa kibali cha kuangalia mpira bure pindi mechi mbalimbali za Ligi hiyo zinapochezwa kwenye Uwanja wa Karume. Je, ni kweli TFF wameshindwa kudhibiti suala hili? Ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kila siku na kushindwa kupata majibu sahihi, ambayo yataniridhisha kuwa shirikisho limeingia makubaliano na soko kuwa wafanyabiashara waangalie mpira bure. Naomba ufafanuzi wa jambo hili mapema ili tujue kama wale wanaoangalia mpira wana ruhusa ya kufanya hivyo au wanafanya kimakosa na kama ni kosa kwa nini hawachukuliwi hatua. Sitaki kuamini kama kweli shirikisho limekubali kuona timu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, kila siku zikitembeza bakuli la kuomba msaada ilhali wanaweza wakatumia viingilio kutatua matatizo yao. Mtanzania tunaomba TFF ichukue hatua za haraka kuhusu jambo hili, maana mficha maradhi kifo humuumbua, hatutaki tufike huko, haitapendeza kuona baadhi ya timu zikishindwa kumudu gharama za uendeshaji kutokana na ukata. | 4 |
KOCHA mpya wa klabu ya Sunderland, David Moyes, amefunguka kwa mara ya kwanza kuelezea maisha aliyokuwa anaishi katika klabu ya Manchester United na kudai kuwa yalikuwa mabaya. Kocha huyo amesema alikuwa hatendewi haki katika klabu hiyo na ndiyo maana alishindwa kuonesha uwezo wake, lakini kwa sasa yupo sehemu sahihi ambayo ataonesha uwezo wake, tofauti na Old Trafford. Kocha huyo alisajiliwa na klabu ya Manchester United kwa mkataba wa miaka sita, lakini hakumaliza mkataba huo kwa kuwa alifukuzwa kwa madai kuwa timu ilikuwa inapata matokeo mabaya. Nafasi ya kocha huyo ikachukuliwa na Louis van Gaal mwanzoni mwa msimu wa 2014-15, lakini na yeye alifukuzwa nafasi hiyo kutokana na mwenendo mbaya wa klabu, ambapo sasa mikoba hiyo ameichukua Jose Mourinho. “Nilikuwa na lengo la kuipeleka United sehemu sahihi, lakini ilishindikana kutokana na mwenendo wa uongozi wa timu kuwa mbaya, nikashindwa kufanya vile ambavyo nilitarajia kufanya. “Nilisaini mkataba wa miaka sita, lakini nilitumikia klabu hiyo kwa miezi 10, kutokana na hali hiyo niliamini kuwa kuna jambo ambalo lilikuwa linaendelea. “Lakini hayo ni maisha ya soka, siku zote ndivyo yalivyo. Kila kocha anakuwa na lengo la kutaka kufanya vizuri akiwa na timu yake, lakini sikuweza kushinda vizuri baadhi ya michezo kutokana na kunyanyaswa. “Ukweli ni kwamba viongozi wa klabu hiyo walikuwa hawanitendei haki, lakini sehemu niliyopo kwa sasa ninaamini nipo mahali salama na nitafanikiwa kufanya vizuri na kurudisha heshima yangu,” alisema Moyes. Hata hivyo, kocha huyo amesema kwamba baada ya kuondoka Manchester United alipata ofa mbalimbali katika klabu kubwa, lakini aliamua kujiunga na Real Sociedad kabla ya kujiunga na klabu ya sasa, Sunderland. Kocha huyo amesema mashabiki wa klabu ya Sunderland watarajie makubwa kwa kipindi cha mkataba wa kocha huyo na anaamini kuwa atafanya ushindani mkubwa dhidi ya makocha ambao wanadhaniwa kuwa watafanya makubwa msimu mpya. “Ni wazi kwamba ligi itakuwa na ushindani mkubwa msimu mpya, kuna makocha ambao wanazungumziwa kuwa watafanya vizuri, lakini wakumbuke hakuna ambaye alijua kama klabu ya Leicester City itachukua ubingwa msimu uliopita, basi hayo yanaweza kutokea katika msimu mpya wa Ligi. “Kila kocha ana lengo la kufanya makubwa, hata mimi nina lengo la kushindana na hao ambao wanadhaniwa wanaweza kufanya makubwa,” aliongeza. | 4 |
CHUO Kikuu cha Dar es Salaam Sehemu ya Mlimani (UDSM), kitawakutanisha watafi ti kuonesha kazi zao za kitafi ti, uvumbuzi, huduma kwa jamii na kubadilishana maarifa kutatua changamoto za kijamii.Mkurugenzi wa Ubunifu na Ujasiriamali Udsm, Dk Ambrose Itika alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia wiki ya tano ya utafiti chuoni hapo inayotarajiwa kuanza Mei 6 hadi 8, mwaka huu.Mkuu wa chuo hicho, Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Kikwete ndiye atazindua wiki hiyo. Dk Itika alisema kaulimbiu ya wiki hiyo ni “Utafiti kwa maendeleo Jumuishi na Endelevu,” ambako chuo hicho kitatumia fursa hiyo kujipambanua katika tafiti ambayo ni mojawapo ya majukumu yake.“Majukumu makuu ya chuo ni kuonesha shughuli za utafiti na uvumbuzi ili kutatua changamoto za kijamii kufikia malengo ya serikali kuelekea uchumi wa kati unaotokana na viwanda na biashara,” alisema.Alisema kupitia wiki hiyo ya watafiti, watatoa fursa ya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi za kitaifa na kimataifa. Kadhalika alisema wiki hiyo itaambatana na kongamano lenye kuwashirikisha wanajopo nguli kutoka mashirika ya umma, binafsi, kimataifa na taasisi za kitaaluma watakaojadiliana kuhusu mada mbalimbali na kutoa mapendekezo mahsusi kwa mustakabali wa maendeleo endelevu nchini Tanzania.Dk Itika alisema katika wiki hiyo, itatumika pia kutambua michango iliyotukuka ya makundi mbali mbali ya wanajumuiya wa chuo katika utafiti, uvumbuzi na ubadilishanaji wa maarifa, ambako Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako atatunuku tuzo hizo katika makundi tisa.Aliyataja makundi yatakayotunukiwa tuzo kuwa ni mradi bora wa mtu binafsi au kikundi, vitengo au idara zilizoingiza kiasi kikubwa cha fedha za utafiti chuoni, watafiti walioingiza kiasi kikubwa cha fedha chuoni na utambuzi wa mtafiti hodari.Maeneo mengine ni katika mtafiti aliyechapisha machapisho mengi zaidi, jarida bora la kitaaluma la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mradi au wazo bora la wanafunzi za uzamili, mradi au wazo bora la wanafunzi wa shahada za awali na huduma bora za jamii au ushauri wa kitaalamu. | 3 |
WANACHAMA wa Yanga bado wanajipa matumaini ya kurejea kwa Mwenyekiti wao wa zamani, Yusuf Manji baada ya kupokewa kwa barua yao.Kupitia mkutano mkuu wa wanachama hivi karibuni waliamua kwa kuandika barua ya kumuomba Manji kurejea na kuendelea na nafasi hiyo, wakiamini ndiye mkombozi wao baada ya kufanya vizuri kabla ya kuachia ngazi mwaka jana hali iliyofanya klabu hiyo kuwa katika mazingira magumu.Tangu kujiuzulu kwa Mwenyekiti huyo aliyekuwa msaada miaka iliyopita ni mwaka mmoja umepita. Hata hivyo, licha ya kupokelewa kwa barua hawajajibiwa.Mwenyekiti wa matawi wa klabu hiyo Bakili Makele amesema waliahidiwa baada ya mfungo wa Ramadhan mambo yatakuwa mazuri hivyo kuwaasa wanachama kuendelea kuwa watulivu.“Tunatarajia atatoa tamko kama atarudi au hatarudi, bado tuna imani kwa sababu ameshapokea barua na dalili za kurejea kwake zipo, tunaendelea kupata ushirikiano wake,” alisema.Makele alisema jambo linaloashiria huenda akarejea ni ushirikiano anaotoa kwenye usajili unaoendelea hivi sasa ambapo kupitia Kamati ya usajili wamekuwa wakiendelea na usajili kimya.Kiongozi huyo wa matawi alifafanua kuwa sasa hivi kuna mambo mengi mazuri yanafanywa na viongozi wa klabu na kuwatoa hofu mashabiki na wanachama wake kuwa silaha za hatari zilizosajiliwa zitatangazwa muda si mrefu.“Mambo ya klabu yanashughulikiwa na viongozi kimya kimya, watu waendelee kuwa watulivu. Manji tuna imani naye atarejea, tunajua ana shughuli zake nyingi akikamilisha atakuja,”alisema.Klabu hiyo imedhamiria kufanya mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji lakini tegemeo lake kubwa imeweka kwa Manji wakiamini ni mtu sahihi kwao. | 4 |
HADI sasa Tanzania haina mgonjwa wala mhisiwa wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na kirusi cha Corona, lakini kutokana na mwingiliano wa kibiashara na kijamii na nchi ya China na Bara la Asia, serikali imechukua hatua kukabiliana na ugonjwa huo ukiibuka.Akizungumza jana na waandishi wa habari katika ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, aliwataka wananchi kutokuwa na hofu, bali waendelee kuchukua hatua za tahadhari katika kujikinga na ugonjwa huo na kutosambaza taarifa zilizothibitishwa na wizara.Ummy amesema kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO), ugonjwa huo tangu mlipuko wake uanze katika mji wa Wuhan katika Jimbo la Hubei, China, Desemba mwaka huu hadi Januari 28, mwaka huu, watu 4,593 wamethibitishwa kuugua duniani kote na kati yao 4,537 na vifo 106 vimetokea China.Alisema ugonjwa huo umesambaa katika nchi 14 duniani ikiwamo Japan, Jamhuri ya Korea, Vietnam, Singapore, Australia, Malasyia, Cambodia, Thailand, Nepal, Sri Lanka, Marekani, Canada, Ufaransa na Ujerumani.Lakini kwa mujibu wa taarifa ya WHO Kanda ya Afrika, kuna washukiwa wanaodhaniwa kuwa na virusi vya ugonjwa huo walioripotiwa katika Bara la Afrika ambao wanaoendelea kufuatiliwa na kufanyiwa uchunguzi katika nchi za Ivory Coast, Ethiopia, Mauritius, Kenya na Zimbabwe.“Wizara inafanya uchunguzi wa wasafiri wote kutoka Bara la Asia kwenye mipaka kikiwamo Kiwanja cha Ndege cha Mwalimu Julius Nyerere, Kilimanjaro, Mwanza na Bandari ya Dar es Salaam.”“Katika kipindi cha wiki mbili zilizopita, wizara imefanya uchunguzi wa raia 1,520 wanaoingia nchini kutoka China na Asia kupitia mipakani na viwanja vya ndege na kuchunguza abiria wa ndege wanaoingia nchini,” alisema.Ummy alisema wizara ina vipima joto 140, vya mkono 125 na vya kupima watu mapigo ya moyo 15, ambavyo vimefungwa na vinatumika katika maeneo yote ya mipakani ikiwamo katika viwanja vya ndege na bandari.Pia aliwataka waganga wakuu wote wa mikao na halmashauri kuchukua tahadhari na kuimarisha ufuatiliaji na mbinu ya kukinga dhidi ya maambukizi katika maeneo yao, ikiwamo mipaka.“Kuandaa maeneo maalumu ya matibabu kwa wagonjwa endapo watajitokeza. Maeneo hayo ni Hospitali ya Mawezi Kilimanjaro, Buswelu Mwanza na Kigamboni mkoani Dar es Salaam.”Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa Wizara ya Afya, Dk Elias Kwesi, alisema ukaguzi kwenye ndege unafanyika kwa umakini mkubwa kutokana na makundi matatu ya ndege zinazotoka moja kwa moja China na Bara la Asia na Mashariki ya Mbali.Alisema ndege zenye hatari kubwa ni za Ethiopia, Kenya na Qatar na Emireti, zenye hatari ya kati ni Tarkish, KLM, Precisioner na hatari ya kawaida ni Tanzania, Msumbiji, Mauritius na Rwanda. | 3 |
BENJAMIN MASESE-MWANZA KATIBU Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),
John Mnyika amemuomba Rais Dk. John Magufuli
kuandaa utaratibu utakaowezesha Watanzania kupiga kura za aina nne, wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2020. Alisema utaratibu huo, utamwezesha mwananchi kupiga kura ya
kumchagua rais, mbunge, diwani na kura ya maoni juu Katiba mpya ambayo itaweka
uhalisia Watanzania wanahitaji Katiba mpya au la. Kauli hiyo, aliitoa jana katika ofisi za Chadema Kanda ya
Viktoria jijini Mwanza, baada ya kusimikwa na wazee wa jadi ya kabila la
Wasukuma na kupewa jina la Chifu la
Malonga, likiwa na maana ya mrekebishaji
yaani kutengeneza mambo yaliyoharibika na kuwa mazuri. Aisema kama utaratibu huo, utashindikana ni vema Serikali
kwa kushirikiana na Bunge kufanya
marekebisho ya mpito kwenye Katiba iliyopo sasa kabla ya uchaguzi mkuu
wa 2020 ili kuwa na tume huru ya
uchaguzi. Alisema muda
uliobaki kabla ya uchaguzi huo,
haiwezekani kukamilika kwa mchakato mzima wa katiba mpya,inawezekana
kufanyika marekebisho ya muda ili kukidhi matakwa ya wananchi yakiwamo kupinga
matokeo ya rais mahakamani na kuwa na tume huru. “Nilipochaguliwa katibu mkuu kuna vipaumbele karibu vitano nilijiwekea
kikiwamo cha kudai tume huru ya uchaguzi, mpya kwa bahati nzuri watanzania
wanayo rasimu ya Katiba mpya ya Jaji Joseph Warioba ambayo kwa namna moja au
nyingine iliharibiwa na watu wachache. “Mara kadhaa Rais Dk. Magufuli amenukuliwa akisema Katiba
mpya siyo kipaumbele chake, wakati kwenye ilani ya chama chake ni miongoni mwa
mambo ambayo waliahidi kuyatekeleza, alipokuja kuzindua Bunge mjini Dodoma
alihiadi, tunashangaa anabadilika,tunapaswa kuchukua tahadhari kwa kumtaka aruhusu mchakato uendelee. “Kwa kuwa muda uliobaki kwenda kwenye mchakato wa uchaguzi
mkuu ni mchache, tunamshauri rais aandae utaratibu utakaowezesha mwananchi
kupiga kura ya kumchagua diwani, mbunge, rais na kupira kura ya maoni juu ya
katiba mpya, hapo tutaona uhalisia kama Watanzania wanahitaji jambo hilo au la. “Sote tunajua Katiba mpya ni ya miaka kuanzia 50 na
kuendelea,kama mchakato huio utakuwa
mgumu, basi kabla ya uchaguzi lazima tufanye marekebisho ya mpito kwenye katiba
yetu ili tupate tume huru ya uchaguzi na
matokeo ya rais kupingwa mahakamani vingine nguvu ya umma itatumika ili kupata
ushindi,”alisema. Akizungumza na viongozi wa kanda hiyo, Mnyika alisema hakuna budi viongozi wa vyama
vya upinzani kuungana pamoja kupeleka muswada bungeni kwa ajili ya kufanya
marekebisho hayo Alisema yapo madai Katiba mpya, ni gharama kubwa, lakini
Rais Dk. Magufuli akikubali kupeleka muswada wa dharura bungeni ili kufanya
marekebisho ya mpito kwenye katiba
iliyopo bila kusubiria mchakato
mzima wa katiba mpya. Mnyika ambaye
alikuwa akishangiliwa kila mara , alisema katiba iliyopo inaweza kuongezwa
vipengele vitatu ambavyo ni tume huru ya
uchaguzi, ibara inayotaka matokeo ya uchaguzi wa rais yapingwe mahakamani na
kifungu kinachosema ili mtu atangazwe kuwa mshindi wa urais lazima awe amezidi
asilimia 50 ya kura zote. Alisema wakati wa uchaguzi mkuu kiwepo pia kipengele cha
kupiga kura ya maoni kuhusu aina gani ya katiba inayotakiwa ili wananchi
waipigie kura wakati wakichagua wabunge, madiwani na rais. Kwa upande wa wazee
waliomsimika Mnyika na kumkabidhi mkuki, ngoma ya asili, kigoda
na kibuyu, walisema kumsimika a na kumpa jina la kichifu ni ishara ushindi wa chama hicho na kushika
dola baada ya uchaguzi Mkuu mwaka 2020. Wazee hao, ni Jakton Katinde, Buluno Zacharia na Mzee Mtani
walisema yapo mambo yaliyoharibika katika uongozi uliopita hivyo
wameamua kumpa jina la Malonja lenye maana ya mrekebishaji ambapo wana imani
atarekebisha baadhi ya masuala amabyo
hayakwenda vizuri. “Hata Nyerere alipokuwa akipigania uhuru wa taifa hili
alikalia kigoda hiki akasema tunataka uhuru wetu, wazungu wote waliogopa na
kutawanyika na wewe kukalia kigoda hiki umepewa nguvu ya kupambana na kushika
dola,” alisema Katinde. | 3 |
YANGA jana ilirejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting. Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, timu zote zilishambuliana kwa zamu lakini ni Yanga iliyoipenya ngome ya ulinzi ya Shooting zaidi.Ushindi huo umeifanya Yanga kufikisha pointi 83 kileleni mwa msimamo ikiwa na tofauti ya pointi moja na mabingwa watetezi Simba, wanaotarajiwa kucheza kesho dhidi ya Mtibwa Sugar. Bao la Yanga liliwekwa kimyani na Pappy Tshishimbi katika dakika ya 16 akiunganisha pasi ya Deus Kaseke na kuujaza mpira wavuni. Bao hilo lilizidi kunogesha mechi baada ya pande zote mbili kushambuliana kwa zamu.Yanga walikosa mabao kadhaa ya wazi ambapo katika dakika ya 30, Heritier Makambo na Raphael Daudi walikosa mabao baada ya mipira yao kugonga mwamba na kurudi uwanjani kabla ya kuokolewa na mabeki wa Shooting. Makambo alipata nafasi nyingine katika dakika ya 59 ambapo akiwa peke yake na kipa akapiga shuti hafifu lililoshindwa kufika golini.Shooting ilibadilika kipindi cha pili na kutawala lakini umakini mdogo wa washambuliaji wake uliwanyima mabao. Timu hiyo nusura iandike bao dakika ya 87 baada ya mchezaji wake Fully Zully shuti lake kudakwa na kipa Clous Kindoki wa Yanga.Ruvu Shooting imebaki nafasi ya 14 ikiwa na pointi 42. Kwenye uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga, Mwadui ililazimishwa sare ya mabao 3-3 na Mbao. Matokeo hayo yanaifanya Mbao kushika nafasi ya 10 kwenye msimamo ikiwa na pointi 44 na Mwadui ni ya 19 ikiwa na pointi 38. | 4 |
SERIKALI haina mpango wa kuvibadili vyuo vya Maendeleo ya Wananchi kuwa VETA. Hayo yamebainishwa jana mjini hapa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Willam Ole Nasha wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Rufiji, Mohamed Mchengerwa (CCM). Mchengerwa alisema katika swali: “Serikali imerejesha vyuo vilivyokuwa vya maendeleo kuwa chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya kusema hayo, alitaka kujua kama serikali haioni umuhimu wa kukibadili chuo cha Maendeleo Ikwiriri FDC kuwa VETA ili kubadili fikra za wananchi wa Rufiji, Kibiti na hatimaye kuleta mwamko wa elimu. Akijibu swali hilo, Waziri Ole Nasha alisema elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi hutolewa katika shule na vyuo katika kiwango na madaraja mbalimbali kulingana na malengo yake. Alisema ngazi ya shule za sekondari, elimu ya ufundi hutolewa kumuandaa mwanafunzi kujiunga na vyuo vya ufundi stadi na ufundi wa kati.“Vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi huandaa mafunzi mchundo na vyuo vya ufundi wa kati huandaa mafundi sanifu. Aidha, vyuo huandaa wahandisi katika fani mbalimbali zinazohusiana na ufundi.” Waziri Ole Nasha alisema vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vilianzishwa kwa lengo la kumsaidia mwananchi kukabiliana na changamoto za kimaendeleo katika mazingira yake kwa kumpatia maarifa na stadi anuai Alisema kwa sasa serikali haina mpango wa kuvibadili vyuo vya Maendeleo ya Wananchi kuwa VETA na badala yake imejikita katika kuviboresha vyuo hivyo kwa kuvikarabati na kuviongezea vifaaa vya kujifunzia na kujifundishia ili viweze kutoa mafunzo bora zaidi. Waziri Ole Nasha alisema awamu ya kwanza ukarabati wa vyuo vya Maendeleo ya Wananchi 20 ipo katika hatua za mwisho za ukamilishaji, na awamu ya pili inatarajiwa kuanza mapema Juni mwaka huu. “ Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Ikwiriri kilikuwa katika awamu ya kwanza na ukarabati umekamilika,” alisema. Aidha, Ole Nasha alisema katika mwaka wa fedha 2019/2020 Rufiji ni miongoni mwa wilaya zilizotengewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya cha VETA. | 3 |
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM KATIKA miaka ya karibuni, Serikali imekuwa ikifanya jitihada za kukaribisha na kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika shughuli za sekta ya fedha nchini. Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora, anasema serikali imechukua uamuzi huo baada ya kuonekana kwa mafanikio makubwa katika matumizi ya teknolojia katika kufanikisha upatikanaji wa huduma mbalimbali. Profesa Kamuzora ameeleza mtazamo huo wa Serikali wakati wa maonyesho ya benki na taasisi mbalimbali zinazohusika na sekta ya fedha, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, hivi karibuni. Wito huo wa Profesa Kamuzora umekuja wakati muafaka kwa kuwa sasa dunia inakwenda kasi katika masuala ya sayansi na teknolojia, huku mataifa yaliyoendelea yakiona asilimia kubwa ya wananchi wake wakitumia njia wezeshi za teknolojia ili kupata huduma za kifedha mahali popote, wakati wote na hivyo kutohitajika kutembea na fedha mifukoni. Miongoni mwa kampuni zilizoshiriki maonyesho hayo ni DataVision International, ambayo imebuni mfumo wa kutengeneza kadi papo hapo na hivyo kuziwezesha taasisi kutoa kadi za aina tofauti zikiwemo za kielektroniki zinazomwezesha mteja kutoa fedha katika mashine za kutolea fedha (ATM), vitambulisho na kadi za huduma mbalimbali zikiwamo za manunuzi. DataVision International wanazishauri taasisi hizo kutumia mfumo wa KadiPap kwani ni rahisi na salama katika kutengeneza kadi. Kwa kutumia mfumo huu taasisi mbalimbali zikiwamo za fedha zinakuwa na uwezo wa kumfungulia mteja akaunti na kumtengenezea kadi yake papo hapo hivyo kuondoa usumbufu kwa wateja. “Itakumbukwa huko nyuma baada ya kujiunga na huduma ya benki mteja alilazimika kusubiri kwa zaidi ya siku saba kupata kadi ya ATM; lakini mfumo huu unaondoa kabisa usumbufu kwani unawezesha kadi kutengenezwa wakati huo huo na kuwa tayari kwa matumizi,” anasema Meneja Bidhaa wa DataVision International, MacLean Mwaijonga. Mwaijonga anaamini kuwa itafika siku Watanzania watatembea bila fedha taslimu mifukoni; hata hivyo ili kufikia hali hii ni lazima kuwapo na kasi ya kutengeneza mifumo ya kuwezesha utumiaji wa kadi za kulipia huduma mbalimbali. “Kwa muda mrefu tumekuwa tukitengeneza kadi mbalimbali zikiwamo za vitambulisho, kufungulia milango au mageti pamoja na zile zinazotumika kuwezesha huduma za kifedha. “Mfumo wa KadiPap unaweza kutumika na benki, vikundi vya kuweka na kukopa (Saccos) na taasisi zingine za kifedha ambazo zinawapa wateja au wanachama wao kadi. Mfumo huu unaweza kutumika kwenye taasisi mbalimbali pia kama za kielimu, kiafya, mifuko ya bima na kadhalika,” anasema. DataVision International imetengeneza mfumo unaotumia kadi za kielektoniki ili kuweza kusimamia na kuwatambua wafanyakazi wa Kampuni ya madini ya Acacia kwa ajili ya kupata huduma ya chakula. “Kabla ya mfumo wetu ambao unaitwa ‘Canteen Information Management System’, Acacia walikuwa wakitumia mfumo wa kutoa karatasi ambazo wakati mwingine ulikuwa unatumika vibaya na wafanyakazi wasio waaminifu na hivyo kuiingiza hasara kampuni kwa kutoa huduma ya chakula hata kwa watu wasiohusika. “Baada ya kuanza kutumia mfumo unaotumia kadi Acacia imeweza kuondokana na changamoto za kuwatambua wafanyakazi, kufahamu wamekula nini na kutunza kumbumkumbu sahihi za malipo kwa ajili ya kuwalipa wakandarasi wanaotoa huduma ya chakula migodini,” anasema. Pamoja na ubunifu ambao kampuni ya DataVision International imekuwa inaufanya katika kuleta ufanisi wa upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa kutumia kadi za kieletroniki. Mwaijonga anasema bado kasi ya ukuaji wa matumizi ya kadi nchini ni ndogo ikilinganishwa na nchi zilizoendelea na hali hii inachangiwa na kukosekana kwa uelewa wa huduma hizo; hivyo elimu zaidi inahitajika kutolewa kwa wananchi. Huduma za kadi kwa ajili ya malipo zina manufaa mengi kwa watumiaji pamoja na taasisi ikiwamo kupunguza muda wa kutoa/kupata huduma, usalama kwa kuwezesha kufanya utambuzi, kupunguza gharama za kutoa huduma kwani kwa njia ya kadi na endapo ikiunganishwa na mawasiliano ya simu mhusika anaweza kutoa/kupata huduma wakati wowote. Pamoja na kwamba bado Watanzania wengi wana mazoea ya kutumia fedha taslimu katika kulipia huduma hali inayowalazimu kutembea na fedha nyingi, changamoto za usalama zinaweza kusaidia kuwafanya waanze kugeukia matumizi ya mifumo ya kieletroniki. “Ni kweli mabadiliko yanachukua muda na hasa yale yanayohusu fedha. Hata mimi wakati mfumo wa kutumia simu za mkononi kutuma na kupokea fedha ulipoingia nchini nilikuwa nina hofu. Hata hivyo, kadiri siku zilivyokwenda nikaanza kuzoea na kuona namna ilivyo rahisi na salama. “Hivyo nawaasa Watanzania wenzangu kuwa sehemu ya mabadiliko haya, mtu akijaribu ataona utofauti. Kwa sababu mtu anayebeba fedha nyingi daima ana wasiwasi. Lakini mtu anaweza kubeba kadi yenye zaidi ya Sh milioni 100 bila mtu wa jirani kujua, na kadi hiyo inamwezesha kufanya huduma yoyote kwa kugusisha tu kwenye mashine,”anasema Naye Meneja Masoko na Uhusiano wa DataVision International, Teddy Qirtu, anatoa wito kwa vikundi vya Vicoba, Saccos na taasisi zingine za fedha kujiunga katika mfumo wa kadi ya kieletroniki uliotengenezwa na kampuni yake ili kuepuka madhara yatakayotokea wakati wa kutembea na fedha nyingi kwa wakati mmoja. | 3 |
Na CHRISTIAN BWAYA MITAFARUKU mingi inayosumbua ndoa ingeweza kuepukika kama wapenzi wasingepuuza dalili za hatari. Mara nyingi dalili hizi huonekana mapema lakini mapenzi huwafanya wapendanao kuzipuuza wakiamini zitaondoka. Madhumuni ya mfululizo wa makala hizi ni kumsaidia kijana anayejiandaa kuingia kwenye uhusiano wa kudumu, aghalabu ndoa, kupata mwangaza wa mambo ya kushughulikia kabla hajala kiapo cha ndoa. Wiki iliyopita tuliangazia masuala kadhaa yanayohusu uaminifu. Tulieleza kwamba haiwezekani kuwa na ndoa imara na mwenzako ikiwa mmoja wenu hana uaminifu. Sura ya kwanza ya uaminifu ni kuishi maisha yenye mipaka, kujua nini sipaswi kukifanya na kipi naweza kukifanya lakini kwenye mazingira fulani. Sura ya pili ya uaminifu ni uwezo wa kulinda urafiki katika mazingira yoyote. Tuliutazama uaminifu kama hali ya kutokuwa na wasiwasi kuwa mwenzako anaweza kukugeuka katika mazingira Fulani fulani. Tulihitimisha kuwa unapoona dalili za mtu kukosa uaminifu kabla ya ndoa, usipuuze. Katika makala ya leo ningependa tutazame kidogo suala la ukomavu. Katika muktadha wa makala haya, ukomavu ni ule uwezo wa kujisimamia na kufanya uamuzi wako mwenyewe bila kutegemea zaidi nguvu kutoka nje. Sina maana ya kutokuhitaji ushauri kwa mtu yeyote bali kuwa na ule uwezo wa kutafakari ushauri unaoupata na kuufanyia kazi pale inapobidi. Upande mwingine wa ukomavu ni ule uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazojitokeza bila kuumiza hisia za wengine. Tunafahamu, ukitaka kujua kiwango cha utu uzima alichonacho mtu tunatazama namna anavyokabiliana na mabaya yasiyo tarajiwa. Ndio kusema, mbali na idadi ya miaka aliyokuwa nayo mtu, ukomavu wake huonekana pale anapoweza kumudu changamoto mbalimbali anazokutana nazo. Mtoto, shauri ya ubinafsi, huhamaki anapokutana na magumu na matokeo yake kuzalisha matatizo mengine. Lakini mtu aliyekomaa anao uwezo wa kushughulikia mambo magumu bila kuyakuza na kuyafanya yazalishe matatizo mengine. Swali ni je, unawezaje kujua ukomavu wa mtu? Je, mtu anaweza kuwa na miaka 40 na bado akashindwa kuwa mtu mzima? Katika kujibu swali kama hili, nikupe kisa kimoja. Idris, kijana wa miaka 33 amemuoa Shadya, mwanamke anayempenda sana. Miezi michache baada ya ndoa yao, Shadya analalamika kutokuwa na mawasiliano mazuri na mama mkwe wake ambaye ndiye mama wa Idris. Tangu akiwa kijana mdogo, Idris alikuwa na ndoto ya kuwa na mke atakayekuwa karibu na mama yake. Taarifa kuwa mke wake Shadya haelewani na mama yake zinamchanganya. Ingawa anampenda sana mke wake Shadya, Idris anaanza kupatwa na wasiwasi na tabia hiyo ya mke wake akiamini ana chuki binafsi na mama yake. Haraka haraka Idris anakwenda kwa mama yake kujaribu kuelewa kulikoni haelewani na mwali wake. Maelezo ya mama yanaonesha namna gani Shadya ni tatizo jipya katika familia. Kichwa cha Idris kinabeba taarifa hizo kama zilivyo kwa imani kuwa mama hawezi kukosea. Hapo ndipo matatizo katika ndoa yanapoanza. Ufa mkubwa unajitokeza kati yake na mkewe. Kubwa ni imani kuwa Shadya si mtu mwema. Hata katika nyakati chache anapofanya maongezi na mkewe, Idris haonekani kuelewa kuwa Shadya naye kwa upande wake anaweza kuwa na hoja za msingi. Imani kuwa hakuna namna mama yake anaweza kuwa upande wa kukosea, inamfanya hata anapozungumza na mkewe awe kwenye upande wa kushutumu na kuonesha makosa. Visa kama hivi vipo kwenye familia nyingi. Mke anakuwa haelewani na wakwe zake wakati mwingine kwa sababu zao binafsi lakini mume hayuko tayari kuvaa viatu vya mke wake. Idris ni mfano wa wanaume wengi wanaojaribu kutatua tatizo kwa kuzalisha tatizo. Badala ya kujenga daraja kati ya mama yake na mkewe bila kutengeneza mtafaruku zaidi, Idris anashughulikia malalamiko ya mke wake kwa kuzalisha mtafaruku mkubwa zaidi. Badala ya kutazama tatizo kwa picha pana, Idris anatumia macho ya mtu mmoja kufanya uamuzi. Kwa upande mwingine, inavyoonekana, Idris anaamini kumpenda mama yake maana yake ni kutokuona dosari yoyote kwake. Ingawa kwa juu juu hili linaweza kutafsiriwa kama busara na utiifu kwa mama, ukweli ni kwamba mtazamo huu unaweza kumfanya Idris akawa kipofu wa hisia za mkewe zinazoweza kuwa sahihi pia. Watu kama Idris huwa ‘hawaondoki nyumbani.’ Wanakuwa tayari kupuuza hisia za wake zao kwa minajili ya kulinda hisia za upande mmoja bila kujipa muda wa kufanya utafiti. Wanasahau kuwa ukomavu ni pamoja na kutokumpendelea mtu Fulani kwa gharama ya kumuumiza mwingine. INAENDELEA Christian Bwaya ni Mhadhiri wa Saikolojia, Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU). Kwa unasihi wasiliana naye kwa 0754 870 815. | 0 |
MWENYEKITI wa Kamati ya Kitaifa ya Maaskofu na Mashehe ya Maadili, Amani na Haki za jamii ya Madhehebu ya Dini nchini, Askofu William Mwamalanga ameonya kuhusu vitendo vywa ukatili nchini ikiwa ni pamoja na utekaji watu, chuki, kiburi na maneno ya uchochezi yenye lengo la kumtenga Rais na wananchi.Akihubiri kwenye usiku wa ibada ya dua iliyohudhuriwa na waumini jijini Dar es Salaam wakiwemo maaskofu na viongozi wa dini katika eneo la Madale ambapo Askofu Mwamalanga alionya kuwa Mungu huwa hashiriki na waovu kamwe.“Ukiwa na tabia za chuki, visasi na hasira dhidi ya mwingine unakuwa wakala wa shetani, huwezi kushirikiana na Mungu na sala, dua na maombi yako ni bure,” alisema.Alisema kuna baadhi ya watu wametumbukia katika kutoa hotuba za chuki, matusi na kejeli zinazochochea kumtenga Rais na Watanzania, jambo ambalo sio sahihi ila ni muhimu kumuombea na kumtakia amani yeye na familia yake yote ili Mungu amuongoze kutenda haki kwa raia wote bila ubaguzi wa aina yoyote.Askofu Mwamalanfa aliwapongeza watu wote wanaokemea vitendo hivyo ambavyo vimekuwa kiini cha chuki miongoni mwa wantanzania, Rais na serikali na kuongeza kuwa kuanzisha mijadala ya kuhamasisha chuki dhidi viongozi ni hatari kwa mstakabali wa amani na ustawi wa taifa.“Ni kweli haikubaliki kwa nchi yetu kuibuka kwa kundi linaloitwa halijulikana lenye nguvu kuliko serikali tena kuliko Watanzania wote ni lazima tulikatae huo sio utamaduni wetu, hii siyo nchi ya kuuana na kuchukiana, nalionya kundi hili mwisho wake umefika limurudie Mungu Mwenyezi kwani uovu huo umefika mwisho wake na saa ya kuacha uovu huo ni leo, kwani uongo wa shetani tayari umejulikana mbele za Mungu …nawaomba watanzania tumutegemee Mungu kwa asilimia 100, chuki na visasi ni dhambi mbele za Mungu,” alisema.Alikemea pia tabia ya baadhi ya watu wanaotumia Bibilia na ushirikina kusaka utajiri kwa kupotosha watu na kueleza kuwa hao nao hawana tofauti na ‘watu wasiojulikana’ kwani nao ni wauaji wa roho za watu.Usiku wa ibada ya dua ulizinduliwa Dar es Salaam kwa kushirikisha maelfu ya waumini wa madhehebu mbalmbali ya kikristo na kiislamu.Dua hiyo itakuwa inafanywa kila mwezi katika kila wilaya hapa nchini na kushirikisha viongozi wote wa kiroho kama yanenavyo maandiko katika Biblia 1Timotheo 2:1-4 | 3 |
Na ADAMA MKWEPU, DAR ES SALAAM ILE hadithi ya mafahari wawili wasiokaa zizi moja iliyoamia katika klabu ya soka ya Yanga kama isipoangaliwa kwa umakini na kutafutiwa ufumbuzi athari zake zinaweza kuja kuighalimu timu hiyo katika michuano inayoshiriki. Ni ukweli husiona na shaka kwamba washambuliaji wawili timu hiyo Amissi Tabwe na Donald Ngoma kwa sasa hawaivu chungu kimoja ikiwa ni takribani miezi miwili tangu waingie kwenye bifu zito. Ngoma na Tambwe ndio safu ya ushambuliaji ya timu hiyo ambayo msimu uliopita 2015/16 ilifanya vizuri zaidi kwa kuwa na jumla ya mabao 38 yakiwa ni mabao mengi kuliko wengine katika Ligi hiyo. Pia wachezaji hao wawili waliweza kuisaidia timu hiyo inyakue Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita. Zaidi ni kwamba Tambwe ni mfungaji bora si msimu uliopita tu bali misimu miwili mfululizo amefanikiwa kuwa bora na kufanya vizuri katika Ligi hiyo. Hata hivyo Ngoma amekuwa katika wakati mzuri na kiwango bora tangu atue kwenye klabu hiyo yenye maskani yake Jangwani. Ngome ameweza kukonga nafsi za mashabiki wa timu hiyo hasa katika michezo ya mwisho ya msimu uliopita pamoja na michezo ya Kimataifa kutokana na juhudi na kipaji chake uwanjani. Kwa sasa kila mmoja aneonekna kuwa bora zaidi ya mwenzake katika timu hiyo kiasi ambacho kimesababisha kutokea chuki miongoni mwao na kusababisha vikao vya mara kwa mara ili kujaribu kuwatuliza. Washambuliaji hao hadi sasa hawapati licha ya uongozi wa klabu hiyo kudai kwamba hakuna kitu kama hicho, lakini ukweli ni kwamba Ngoma anaoenekana kuwa na chuki zaidi dhidi Tambwe. Chuki hiyo alihidhihilisha wakati wakiwa mazoezini walipoweka kambi hoteli ya Rui nchini Uturuki siku moja kabla ya kucheza na TP Mazembe, mchezo ambao Yanga ilifungwa bao 1-0. Ngoma kwa ghadhabu alimvamia na kumpiga Tambwe na kusababisha kushonwa nyuzi tatu kichwani kutokana na kile kilichodaiwa ni bifu la muda mrefu. Mzimbabwe huyo wakati akifanya tukio hilo alieleza kwamba mwenzake alikuwa akipendelewa zaidi na kocha wa timu hiyo. Hata hivyo kitendo hicho kiliibua maswali mengi ambayo hayakuwa na majibu si mimi na wewe bali hata baadhi ya viongozi wa klabu hiyo hawajafahamu namna ya kufanya ili kuwatuliza mafahali hao. Kocha Mkuu wa timu hiyo Hans van Puijm amedaiwa kuitisha vikao kila kukicha hili kuondoa chuki miongoni mwao lakini ilionekana kazi bure. Tayari Tambwe ametamka waziwazi kwamba hatoweza kumsamehe mchezaji mwenzake licha ya Pluijm kutumia muda mwingi kuondoa hali hiyo. Kwa sasa washambuliaji hao hawazungumzi wala kusalimiana kama ilivyokuwa awali ambapo waliweza hata kuombana pasi wakiwa uwanjani na kushirikiana katika kuisaidia timu hiyo. Kukomaa kwa bifu hilo hadi uwanjani ni nadra kwa sasa kumuona Tambwe akimwomba pasi Ngoma au kumsemesha wakiwa uwanjani. Kimsingi ugomvi huo umeonekana kuigawa timu hiyo na kusababisha kuwepo wafuasi upande wa Tambwe na Ngoma. Mpasuko huo uliozalisha makundi mawili ya wazawa na wazimbabwe umepunguza hamasa na hali ya kujituma ndani ya timu hiyo. Kufanya vibaya kwa timu hiyo katika michezo ya kimataifa kunasababishwa na vitu vingi ikiwemo kitendo cha wachezaji kujigawa ndani ya timu hiyo. Licha ya ujio wa Obrey Chirwa ili kuongeza nguvu katika safu hiyo, inahitaji zaidi ushirikiano wa Ngoma na Tambwe ili kuimarisha safu hiyo. Bado Tambwe na Ngoma wanayonafasi ya kuendelea kufanya vizuri kama hawatakuwa na bifu kutokana na umahiri wao wanapokuwa uwanjani. | 4 |
Ramadhan Hassan -Dodoma SERIKALI kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamin Mkapa imemwaga ajira
307 kada ya afya katika halmashauri 68 kuimarisha huduma za Ukimwi, kifua
kikuu, malaria na magonjwa ya milipuko kama corona. Pia Serikali ipo hatua za mwisho kukamilisha ajira za wataalamu
wengine wa afya 80 watakaopangiwa kufanya kazi katika hospitali za rufaa za mikoa
ya Shinyanga, Mara, Geita, Simiyu, Kagera, Kigoma, Tabora, Dodoma, Katavi na
Mwanza. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alipokuwa akizungumza na waandishi
wa habari akiongozana na Naibu wake, Dk. Faustine Ndugulile na Katibu Mkuu, Dk.
Zainabu Chaula. Ummy alisema taratibu za ajira kwa wataalamu wa afya 307 zimekamilika
ambapo lengo kuu ni kuongeza nguvu katika sekta ya afya ili kuimarisha jitihada
za kupambana na magonjwa ya Ukimwi, kifua kikuu, malaria pamoja na magonjwa ya
milipuko kama Covid-19. Alisema wataalamu hao wamepangiwa kufanya kazi katika mamlaka za
Serikali za mitaa 68 zilizopo mikoa 11 nchini. Ummy alisema kupitia mchakato huo wa ajira, kada sita za wataalamu wa
afya zimenufaika na kibali hicho ambazo ni kada ya wauguzi wenye cheti 59, wauguzi
wenye Diploma 30, maofisa tabibu 73, maofisa tabibu wasaidizi 100, wataalamu wa
maabara ngazi ya cheti 25 na ngazi ya diploma 20. | 0 |
Na DERICK MILTON-SIMIYU Zaidi ya wakazi 4000 kutoka katika kata nane za Wilaya ya
Bariadi Mkoani Simiyu, wamejitokeza kwa wingi katika shule ya msingi Ngulyati,
kwa ajili ya kupatiwa bure huduma mbalimbali za afya kutoka kwa madaktari bigwa
50. Akielezea lengo la zoezi hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya
Kiislamu (The Islamic Foundation),
Mubaraka Said amesema kuwa wameamua kutoa bure huduma hizo kwa wananchi ikiwa
ni moja ya malengo makuu ya kusaidia jamii kwa kuwaunganisha watanzania bila
kujali dini wala kabila zao. “Taasisi yetu imeamua kutoa huduma hii kwa kila jamii, hii ni
moja ya malengo tuliyojiwekea ya kusaidia jamii inayotuzunguka, afya ni muhimu,
tofauti zetu katika dini na kabila haziwezi kututenganisha tukashindwa
kusaidiana katika mambo ya muhimu kama haya,” amesema Mubaraka. Wananchi waliohudhuria katika zoezi hilo wametoka katika kata za Gamboshi, Kilalo, Sakwe, Ngulyati, Mwasubuya,
Kasori, Mhango na Itubukilo ambapo zipo ndani ya Wilaya ya Bariadi. Madaktari waliohusika katika utoaji wa huduma hiyo wametoka katika
Mkoa wa Mwanza, Shinyanga na Simiyu kwa ufadhiliwa wa taasisi hiyo ya Kiislamu chini
ya uratibu wa kampuni ya pamba ya Allience Ginnery iliyopo Wilayani humo. Kwa upande wake meneja wa kampuni ya Allience, Boaz Ogola, amesema
wao kama wawekezaji wamekuwa wakitoa huduma mbalimbali kwa jamii ikiwa ni moja
ya njia ya kudumisha ushirikiano na kurejesha faida kwa jamii inayoipata huduma
ya kampuni yao. | 0 |
Na ASHA BANI-ZANZIBAR KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema kukaa kwake kimya kuna kishindo kikubwa kinakuja visiwani Zanzibar. Maalim Seif ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa visiwani humo, alisema kamwe hatorudi nyuma, kwani hajashindwa na wala haitotokea kushindwa katika maisha yake. Kauli hiyo aliitoa jana mjini Unguja, alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani, ambapo pamoja na mambo mengine alisema umaskini sasa umekuwa ukiwatesa wananchi katika kila eneo. Katika uchaguzi huo CUF inawakilishwa na mgombea wake Abdulrazak Khatib Ramadhan ambaye anapambana vikali na mgombea wa CCM, Juma Ali Juma. Maalim Seif ni kama alikuwa akijibu mapigo ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdurhamn Kinana ambaye mwishoni mwa wiki alisema kuwa kiongozi huyo anazungumza hali ya kuwa hajui lolote kinachoendelea katika nchi wala katika chama chake. “Sasa nawaambieni musinione kimya, kimya kikuu kina mshindo mkubwa wala usidhani kuwa tumeshaachia hapana bado kabisa tunaendelea kupigania haki yenu na haki Inshallah haipo mbali na mimi niwaambieni vijana sijashindwa na sitoshindwa. “…na kama itatokea bahati mbaya nishindwe nitawataarifuni mchukue uamuzi wenu lakini sitegemei kufika huko kwani mambo haya yana miiko yake,’’ alisema Maalim Seif. Akizungumzia hali ya umaskini nchini alisema tangu uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, ulipoingia madarakani kwa kile alichodai kwa kutumia mabavu hali ya umaskini imeendelea kuwatesa wananchi. Alisema hali hiyo inachangiwa na uongozi kufanya mambo yasiyokuwa na tija ambapo kwa kushirikiana na kiongozi mstaafu wa Serikali iliyopita walifanya mapinduzi na kubatilisha matokeo ya uchaguzi yaliyofanywa na Wazanzibari waliyoyafanya Oktoba 25, mwaka 2015. “Lakini kilichotokea mwaka juzi sasa Serikali imekuwa ya dhulma wale wenye ajira wanapokonywaa ajira zao ikiwemo kuwaondosha wafanyabiashara darajani, Kijangwani na sasa wanakwenda Michenzani jambo ambalo ni hatari kwa Taifa hili,’’ alisema Maalim Seif. Katibu Mkuu huyo wa CUF ambaye alikuwa mgombea urais katika uchaguzi uliopita, alisema pamoja na hali hiyo lakini bado suala la mafuta na gesi limekuwa na upungufu hasa kupitia sheria yake ambapo sasa kunaifanya Zanzibar kuwa kama manispaa. Lowassa akumbusha ya 2015 Naye aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), aliyeungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) Edward Lowassa, alimpongeza Maalim Seif kwa kumwalika na jinsi alivyokuwa mvumilivu katika mambo yote wanayomfanyia. Alisema Maalim Seif alimshinda aliyekuwa mgombea urais wa CCM, Rais Dk. Ali Mohamed Shein kwa wastani wa kura 16,000. Kutokana na hilo aliwashukuru vijana waliosikia wito wake wa kutofanya vurugu baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo kwani kama wangefanya hivyo kulikuwa na hatari ya kupoteza maisha. Akizungumzia suala la njaa alisema ni ajabu kwa Rais aliyepo madarakani kubeza suala hilo. Lowassa alisema kuwa wakati wa utawala wa Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, hasa pale nchi ilipokubwa na baa la njaa, alisema yupo tayari kuzungumza na makaburu ili kuweza kukabiliana na baa hilo lililoikumba nchi kwa wakati huo. Alisema ni lazima kuhakikisha katika uchaguzi mbalimbali kunakuwa na ushindi na kila mmoja akatae azuie wizi wa kura kama uliotokea 2015. “Lazima kukataa kuibiwa kura ni lazima kukataa kutiwa hofu na kutishwa hii ni nchi yetu sote tufuate sheria na uchaguzi ujao ni lazima kushinda na viongozi wanaopambana ni lazima kuungwa mkono kama ilivyokuwa kwa Maalim Seif ni mfano wa kuigwa,’’ alisema Lowassa. Naye Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Mazrui alisema wanaingia katika uchaguzi huo bila kuwa na ruzuku lakini hadi sasa tayari Sh milioni 20.4 zimepatikana kutoka kwa wanachama wenyewe. Aliyashukuru majimbo yaliyochanga ikiwa ni pamoja na Nungwi, Makunduchi, Mtoni, Magomeni, Kikwajuni, Konde, Chambani, Chakechake, Chonga, Bububu na Ole. Naye Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi Zanzibar, alisema wataendesha kampeni kistaarabu tofauti na wa upande wa pili ambao ni CCM wanaorusha maneno badala kueleza sera. Alitoa ratiba za kampeni hiyo ambapo Januari 11 atakuwepo Mbunge wa Singida Tundu Lisu na Januari 15 Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro atakuwa mgeni rasmi. Sumaye na siri ya kuhama Mwandishi wetu, Johanes Respichius anaripoti kutoka Dar es Salaam kuwa, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, amesema kuwa hakukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutaka cheo bali alitoka ili kuisaidia Chadema kuchukua nchi. Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam wakati akimnadi mgombea udiwani wa chama hicho wa Kata ya Kijichi, Federick Rugaimukama. Alisema lengo la kuhamia Chadema haikuwa kwa ajili ya kupata cheo na kwamba hakuna cheo kingine kikubwa alichokitafuta kwani tayari amekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 cheo ambacho ni kikubwa sana. “Nimekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 kwahiyo ni cheo gani nilichokitafuta Chadema, nimekuja huku kuunganisha mashambilizi ya kukitoa CCM madarakani na ninaamini ifikapo 2019 mitaa yote tutaichukua hivyo hivyo 2020 katika uchaguzi wa wabunge na urais tutashinda kwa kishindo,” alisema. | 3 |
TAMASHA la Utamaduni la Afrika Mashariki (JAMAFEST) linaanza leo kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam kwa matembezi na burudani za aina yake huku kesho ikiwa ndio uzinduzi rasmi utakaoongozwa na Rais John Magufuli kwenye uwanja wa Uhuru. Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye semina fupi kuelezea tamasha hilo Msemaji Mkuu wa Serikali Dk Hassan Abbas alisema ni heshima kwa Tanzania kuandaa kitu kama hicho ikiwa ni siku chache zimepita ikitoka kuandaa mkutano wa 39 wa Jumuiya ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).Alisema ni fursa kwa watanzania na wasanii kuonyesha Utamaduni wa Afrika ili kulinda urithi wa nchi lakini pia, akisema kutakuwa na mambo mengi mazuri ikiwemo maonesho ya mavazi, michezo ya jadi, burudani na vyakula vya kiutamaduni.“Tamasha ni bure halina kiingilio tunawahimiza watanzania kujitokeza kwa wingi kufurahia maonesho mbalimbali na burudani zitakazotolewa na wasanii,”alisema na kuongeza kuwa serikali imejipanga vizuri kwa kila kitu ili mambo yaende kama yalivyokusidiwa.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya kitaifa ya maandalizi ya Jamafest Joyce Fisoo alisema matembezi ya leo yataanzia Tandika, Chuo cha Bandari, Chang’ombe Polisi na Temeke mwisho ambapo kote huko kutakuwa na makundi kutoka Tanzania, Kenya, Rwanda, Uganda na Burundi watakaongozwa na burudani ya muziki wa singeli. Alisema idadi ya washiriki wa Tanzania ni zaidi ya 1000 imekuwa kubwa kuliko ilivyotarajiwa na bado kuna vikundi vinaendelea kujitokeza kuomba ushiriki hivyo wanafikiria namna ya kuwaingiza, ikifuatiwa na Kenya iliyoleta washiriki 612, Uganda 201, Burundi 179 na Rwanda 125. | 4 |
WAKAZI wa Kijiji cha Buigiri Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma wamemwomba Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kuishinikiza ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashuri ya Chamwino itoe kibali cha kuendeleza makazi yao.Wakazi wa eneo hilo wamezuiwa kwa takribani miaka kumi sasa wasiendeleze maeneo yao. Kilio hicho cha wakazi hao kilitolewa mbele ya uongozi wa kijiji akiwemo diwani wa kata hiyo, Keneth Yindi (CCM) kwenye mkutano ambao watumishi wa halmashauri ya Chamwino idara ya ardhi walialikwa lakini hawakuhudhuria.Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye mkutano huo kwa masikitiko makubwa kutokana na watumishi hao ya kutohudhuria, wamemwomba waziri huyo mwenye dhamana na ardhi kuishinikiza halmashauri hiyo ili waweze kupimiwa viwanja na waweze kujenga nyumba za kisasa.Timoth Jabari kutoka mtaa wa Lusinde alisema kuwa tangu mwaka 2009 wafanyiwe tathimini ya kupimiwa viwanja hawajaoneshwa viwanja, badala yake, kilichofanyika ni kuzuiliwa kufanya shughuli zozote za kuendeleza maeneo.Magreth John anayeishi mtaa wa Chang'ombe amesema kuwa ofisi ya mkurugenzi kupitia idara ya ardhi imekuwa ikitoa ahadi za uongo kwa muda wote huo.Amesema kutokana na ahadi hizo hewa wanamuomba waziri mhusika kuingilia kati zoezi hilo la kuonyeshwa maeneo ya kujenga.Diwani wa kata hiyo, Keneth Yindi akizungumza na wakazi hao alisema anasikitishwa na kitendo cha watumishi wa ardhi kushindwa kufika kutoa majibu.Yindi amesema pamoja na watumishi hao kutohudhuria kwenye vikao mbalimbali vinavyotakiwa vya wakazi hao atahakikisha anawasiliana na waziri huyo ili aweze kutatua tatizo la wakazi hao ili nao kuonyeshewa maeneo yao. | 3 |
LONDON, UINGEREZA KANSELA anayeshughulikia kitengo cha ukusanyaji kodi na kudhibiti matumizi nchini Uingereza, Sajid Javid amesema hatarajii Uingereza kuyumba kiuchumi baada ya takwimu kuonyesha kuwa uchumi umeshuka kwa asilimia 0.2 kati ya Aprili na Juni. Javid aliyasema hayo baada ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini humo kueleza kuwa uchumi umeshuka kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2012. Taarifa hizo zimekuja katika wakati ambao suala la Brexit likiwa limeleta sintofahamu huku baadhi ya viwanda vikifungwa kikiwamo kile cha magari. Tayari takwimu hizo ikiwa ni pamoja na kutikisika kwa paundi ya Uingereza kumeimeibua hofu ya kushuka kwa uchumi. Paundi ya Uingereza imetikisika kwa miezi 31 sasa dhidi ya dola kwa 1.2056, wakati dhidi ya Euro ikishuka kwa 1.0768. Rob Kent-Smith, ambaye ni kiongozi wa GDP, alisema uzalishaji wa viwanda umeshuka na sekta ya ujenzi nayo imedhoofika. Baadhi wanaona kuwa kushuka huko kwa uchumi kumechangiwa na mchakato wa Brexit jambo ambalo pia limegusiwa na Sajid. “Ni kweli kuna biashara ambazo zinaguswa na Brexit wakati ambapo maamuzi yanafanyika,” alisema Sajid. Alisema hakuna mtu ambaye atashangazwa na takwimu hizo. Takwimu hizo zimekuja katika wakati ambao tayari dalili za kushuka kwa uchumi zilianza kuonekana. Kwa mfano takwimu zilizotolewa jana zilionyesha kuwa bidhaa za viwandani za Ufaransa zilishuka kuliko ilivyotarajiwa mwezi Juni. Pamoja na hayo Javid anasema “Hiki ni kipindi kigumu katika uchumi wa dunia, huku ukuaji wa uchumi ukionekana kushuka katika mataifa mengi,” alisema. | 2 |
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019 kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza. “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake. | 5 |
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama amewataka waajiri wote nchini kutonyanyasa wanawake katika masuala ya kazi, ili kuwa na usawa maeneo ya kazi.Alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipofungua semina ya siku moja ya viongozi wanawake kutoka vyama mbalimbali vya wafanyakazi nchini, walipokutana kujadili masuala yanayowahusu wawapo kazini ikiwemo haki na wajibu wao iliyofanyika Jijini Mbeya. Alieleza kuwa waajiri hawana budi kubadili mitazamo hasi iliyopo katika jamii ya kuona wanawake ni viumbe dhaifu, wenye majukumu mengi yanayoweza kukwamishi jitihada zao wawapo kazini, badala yake wawaone kuwa ni viungo muhimu katika kuchangia uzalishaji na maendeleo nchini.“Mchango wa wanawake ni mkubwa endapo utatambuliwa na kuthaminiwa katika nyanja zote za ukuaji wa uchumi, hivyo ni vyema maeneo ya kazi waajiri watimize wajibu wao kwa kundi hili kwa kuzingatia sheria zilizopo na wasinyanyaswe,”alisisitiza. Alisema jitihada za serikali ni kuhakikisha inasimamia vyema sheria na taratibu za kazi nchini kwa kuliangalia kundi hilo ili kuwa na waajiriwa wenye kuzingatia usawa wa kijinsia.“Ninakemea vitendo vya unyanyasaji wa haki za wanawake kazini ikiwemo kukoseshwa haki zao, vyama hivi vya wafanyakazi viendelee kuleta tija katika kukemea matendo hayo,”alisema.Aidha, aliwataka wanawake kuendelea kuvitumia vyama vya wafanyakazi kama jukwaa maalumu la kueleza na kutatua changamoto zao. Aliongezea kuwa, pamoja na changamoto wanazokutana nazo wanawake hawana budi kujiendeleza kielimu ili kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yaliyopo katika masuala ya kazi.Naye, Rais wa Shirikizo la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Tumaini Nyamhokya alielezea umuhimu wa kuendelea kuliinua kundi hilo la wanawake ili kuwasaidia katika kupata haki na usawa kwenye maeneo yao ya kazi. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa TUCTA, Rehema Ludanga alieleza kuwa ni wakati sahihi kuendelea kuchangamkia fursa za maendeleo, ikiwemo uanzishwaji wa viwanda vya wanawake vitakavyosaidia kuondokana na hali ya utegemezi na kuchangia katika ongezeko la uzalishaji nchini. | 3 |
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru), inatarajia kuwafikisha mahakamani askari sita wa Jeshi la Polisi na watendaji watatu wa vijiji wilayani Igunga, baada ya kuomba rushwa ya Sh milioni nane.Akizungumza na vyombo mballimbali vya habari ofisini kwake, Kaimu Kamanda wa Takukuru mkoani Tabora, Musa Chaulo alisema kwamba watu hao watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika . Alisema kwamba watendaji hao wa serikali, walimuomba rushwa mzee Ngaka Mataluma Fale (95) baada ya kumkamata, wakimtuhumu kuwa anajihusisha na tiba asilia bila kibali, kukutwa na mfupa unaodaiwa kuwa wa binadamu, kumiliki silaha za moto, kukutwa na mafuta ya simba, ngozi ya kenge na kukutwa na bangi.Chaulo alisema baada ya Fale kukosa kiasi hicho cha fedha, alitakiwa kuuza ng’ombe ili apate Sh milioni nane kwa ajili ya kutoa hongo kwa maofisa waliomkamata. Aliongeza kuwa Takukuru ilifanikiwa kukamata ng’ombe 11 wa Fale katika Mnada wa Igunga kwa wanunuzi, waliokuwa wakijiandaa kuwasafirisha kwenda Arusha.Alisema baada ya kuwakamata, imewarajesha kwa mhusika. Katika hatua nyingine, Kaimu Kamanda wa Takukuru mkoani Tabora Chaulo alisema katika robo iliyoishia Juni mwaka huu, Takukuru imefuatilia na kukagua miradi 40 ya maendeleo, yenye thamani ya Sh bilioni 9.285. Alisema kati ya miradi hiyo, saba inahusu sekta ya elimu, afya na ujenzi na ina thamani ya Sh bilioni 1.570. Miradi hiyo inafanyiwa uchunguzi. | 3 |
JESHI la Polisi limemkamata na kumpeleka gerezani kutumikia kifungo cha miaka mitano, Ofi sa Mtendaji wa Kijiji cha Lomwe wilayani Mwanga, Mussa Mteti baada ya awali kutoroka.Mteti alishitakiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa makosa matatu lakini alitoroka wakati kesi ikiendelea Mahakama ya Wilaya ya Mwanga. Akitoa taarifa hiyo, Mkuu wa Takukuru mkoani hapa, Holle Makungu, alisema mshitakiwa alikuwa na kesi Namba CC.63/2017 kwa makosa matatu ambapo mawili kati yake ni ya kufanya ubadhirifu kinyume cha kifungu cha 28 cha Sheria ya Takukuru namba 11/2017. Kosa la tatu ni kughushi muhtasari wa Kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Kijiji cha Lomwe na kupata Sh 270,000 kinyume cha sheria.Makungu alisema wakati kesi ikikaribia kutolewa hukumu, Mteti alikimbia na kumlazimu Hakimu wa Mahakama ya Wilaya, Mariam Lusewa kutoa hukumu wakati mshtakiwa akiwa hayupo mahakamani hapo.Awali akisoma hukumu hiyo, Oktoba 31, mwaka huu, Hakimu Lusewa alimtoza mshtakiwa faini ya Sh milioni mbili au kifungo cha miaka mitano kwa kosa la kwanza la ubadhirifu na kosa la pili kifungo cha miaka mitano au kulipa faini ya Sh milioni tano.Katika kosa la tatu la kughushi, alitakiwa kwenda jela miaka mitano, na kwamba adhabu zote zinakwenda kwa pamoja hivyo mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka mitano gerezani. Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa Takukuru mkoani hapa, Makungu alisema taratibu za kumpeleka Mteti gerezani kutumikia kifungo chake zimekamilika na ameanza adhabu yake. | 3 |
Na JUDITH NYANGE, MWANZA MFANYABIASHARA raia wa China, Maihaimiyan Mai (33) mkazi wa mtaa wa Mahina Kata ya Mhandu wilayani ya Nyamagana ameuawa kwa kupigwa risasi kifuani nyumbani kwake na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi ambao pia walijeruhi watu wengine watatu na kupora Sh milioni 1.1. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Augustino Senga, alisema tukio hilo lilitokea Novemba 27, mwaka huu usiku wakati Mai akitoka kwenye shughuli zake za biashara. Alisema wakati Mai alipokuwa akiingia kwenye lango la nyumbani kwake alikutana na watu watatu waliovamia nyumbani kwake huku mmoja kati yao alionekana kuwa na silaha ambaye alifyatua risasi moja iliyompiga kifuani na kufariki dunia papo hapo. “Majambazi hao walimshambulia kwa kumpiga na rungu sehemu mbalimbali za mwili, Ayoni Mai (29) ambaye ni mdogo wa marehemu, pamoja na mke wake Christina Kinyonge na kuwapora Sh miloni 1.1 na simu mbili za mkononi. “Pia walimjeruhi mlinzi wa nyumba hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Pascal (35) kwa kumpiga risasi iliyomparaza kisogoni wakati akitaka kuruka ukuta na kukimbia. “Majeruhi wote watatu wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando wakiendelea kupatiwa matibabu na mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi, ” alisema Senga. Senga alisema jeshi la polisi linawasaka watuhumiwa wote waliohusika katika tukio hilo. Aliwataka wakazi wa Mkoa wa Mwanza kutoa ushirikiano kwa jeshi la hilo kuhusu taarifa za wahalifu hao waweze kuwakamata na kufikishwa katika vyombo husika kwa hatua za sheria. | 3 |
MWANAFUNZI wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Makoteni Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Bimwana Saleh (12) amekufa kwa kuliwa na mamba katika mto Ligoma wakati akifua nguo na mama yake.Mkuu wa wilaya ya Tunduru, Mkoani Ruvuma, Juma Homera amemuagiza ofisa wanyamapori wa wilaya hiyo kumuua mamba huyo ili kuwanusuru wananchi na tishio la kundelea kujeruhiwa na kuuawa na mamba.Homera amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Makoteni muda mfupi baada ya kuitembelea familia ya Mtoto Bimwana Salehe (12) aliyepoteza maisha baada ya kujeruhiwa na mamba na kutoa pole kwa wafiwa.Aidha, Homera aliwataka wakazi wa kitongoji hicho kuchukua tahadhari na kujenga tabia ya kwenda wakiwa katika makundi wanapokwenda kuchota maji au kufua katika mto huo.Alisema utaratibu wa kwenda watu wengi kwa pamoja mtoni utawasaidia kuokoana endapo ikitokea mmoja wao kuvamiwa.Homera aliwataka wazazi na walezi katika kata hiyo kuacha taratibu za kuwatuma watoto wadogo kwenda kufanya shughuli zozote katika mto huo.Mtendaji wa kijiji cha makoteni Ajili Mbemba alimueleza mkuu wa wilaya kuwa watu wawili wamekwishapoteza maisha na wengine watano walijeruhiwa kwa kushambuliwa na mamba katika eneo hilo katika kipindi cha Julai 2018 hadi Februari mwaka huu.Kwa mujibu wa Mbemba waliopoteza maisha ni Furaha Mtindinganya (15) aliyekufa mwanzo mwa mwezi Januari mwaka huu na Bimwana Hashim aliyepoteza maisha Februari 26 mwaka huu.Aidha Mbemba aliwataja waliojeruhiwa na mamba hao na kusababishiwa vilema vya maisha katika eneo la mto huo kuwa ni Shabilu Mohammed (8), Muhdini Dhabiti(29), Katrimu Juma (11), Saidi Issa (19) na merina Omari (15).Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani wa kata hiyo Abbas Ngajime walioomba serikali kuangalia uwezekano wa kuwapunguza mamba hao ili wananchi waweze kuishi kwa amani.Akizungumzia hali hiyo Kaimu Ofisa Wanyamapori wa Wilaya ya Tunduru Limbega Ali pamoja na kukiri kuwepo kwa matukio hayo alisema kuwa tayari amekwishatuma askari wenye silaha kwa ajili ya kwenda kumsaka na kumuua mamba huyo ili asiendelee kuleta madhara kwa watu. | 3 |
Fedha hizo zilikusanywa mwezi Machi. Ofisa Uhusiano wa Manispaa hiyo, Sebastian Mhowera alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam leo.Alisema kipindi cha miezi mitatu tangu kuanzishwa kwa huduma hiyo, kimewasaidia kupata mapato haraka na kwamba wamekusanya Sh milioni 339 katika kodi ya majengo, tofauti na mwaka jana ambapo walikusanya Sh milioni 126."Ushuru wa masoko umeongezeka kwa asilimia 20 ya lengo la kila mwezi, hivyo ni mafanikio makubwa tuliyoyapata kwa kipindi kifupi sana," alisema Mhowera.Aliongeza kuwa katika ada ya kuchangia huduma za afya, imeongezeka kutoka Sh milioni 45 hadi Sh milioni 69. Awali, ongezeko la mapato lilizidi bajeti ya mwaka iliyotakiwa kukusanywa, kwani bajeti za huduma za jiji zimezidi kwa asilimia 18.“Napenda kuwahakikishia wananchi wa Kinondoni kuwa manispaa itazidi kuboresha huduma zake ili kufikia malengo yaliyokusuidiwa," alisema.Mhowera alisema huduma hiyo mpya, inatolewa kupitia mfumo wa E-payment System, ambayo itamwezesha mwananchi kulipa kodi yake muda wowote. | 5 |
ZAINAB IDDY NA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM UCHAGUZI Mkuu wa klabu ya Yanga unafanyika leo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam huku timu hiyo ikitarajiwa kuondoka kesho kwenda Uturuki kwa ajili ya kuweka kambi kujiandaa na mchezo wake na Mo Bejaia. Mchezo huo wa hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, unatarajiwa kuchezwa Juni 19 nchini Algeria. Uchaguzi huo unafanyika baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Baraza la Michezo Taifa (BMT), kuwataka wafanye uchaguzi ndani ya mwezi huu baada ya kutofanya hivyo kwa miaka miwili tangu walipoingia madarakani. TFF ilipanga uchaguzi wa Yanga ufanyike Juni 25 mwaka huu na ilianza kutoa fomu lakini siku chache baadaye tangu TFF itangaze zoezi la uchukuaji fomu, Yanga nao wakatangaza kufanya uchaguzi Juni 11 mwaka huu. Hata hivyo, Jumanne iliyopita TFF ilikutana na viongozi wa Yanga na kuweka mambo sawa na ndipo shirikisho hilo lilipoubariki uchaguzi huo utakaofanyika leo. Katika uchaguzi huo nafasi zinazowaniwa ni Mwenyekiti, makamu mwenyekiti na wajumbe wa kamati ya utendaji. Miongoni mwa wanaowania nafasi hizo katika nafasi ya ujumbe ni Ayoub Nyenzi, Salum Mkemi, Bakari Malima, Godfrey Mheluka na Lameck Nyambaya. Wengine ni David Ruhago, Sylvester Haule, Pascal Laizer, Samwel Lukumay, George Manyama, Hussein Nyika, Beda Tindwa, Tobias Lingalangala, Athuman Kihamia, Mchafu Chokoma na Sizi Lyimo, ambaye ni mwanamke pekee. Makamu mwenyekiti ni Tito Othoro na Clement Sanga huku aliyekuwa mwenyekiti wa timu hiyo akitetea kiti chake. Wakati huo huo, wapinzani hao wa Yanga, Mo Bejaia imemtangaza Nacer Sandzak kuwa kocha mpya. Kwa mujibu wa mtandao wa klabu hiyo, Rais wa klabu hiyo, Zahir Attia, amefanikiwa kupata saini ya kocha huyo hivi karibuni ambaye alikuwa kiungo wa zamani wa timu ya JSKabylie Kamel Yesli. Kocha huyo ameahidi usajili mkubwa ndani ya klabu hiyo kabla ya mchezo dhidi ya Yanga. Hata hivyo, tayari wachezaji wawili wa nafasi ya kiungo, Zidane Mebarakou na Mouhamed Ndoye, watakosa mchezo dhidi ya Yanga kutokana na kuwa na kadi mbili za njano. Mchezo huo unatarajia kuchezeshwa na mwamuzi kutoka Morocco, Bouchaib Al-Ahrach na kusaidiwa na Achik Reddouane na Youssef Mabrouk. | 4 |
AZAM FC jana ilikata tiketi ya nusu fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho la Azam baada ya kuifunga Kagera Sugar kwa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Kaitaba,Kagera.Katika mchezo huo bao pekee lililoifanya Azam kusonga mbele liliwekwa kimiani na Joseph Mahundi dakika ya 79 baada ya kuwatambuka mabeki wa Kagera na kuachia shuti hafifu lilomshinda mlinda mlango wa Kagera Jeremia Kisubi. Azam sasa inaungana na timu za Lipuli FC na KMC kufika hatua hiyo. Robo fainali ya mwisho inatarajiwa kuchezwa leo kati ya Yanga na Alliance.Na baada ya kupata ushindi huo Azam wanatarajiwa kukutana na KMC, kwenye hatua inayofuata ya nusu fainali. Mchezo wa jana ulianza kwa kasi kubwa huku kila timu ikicheza kwa umakini mkubwa wakihofia kuruhusu bao la mapema kwenye lango lao lakini mpaka mapumziko hakukuwa na timu iliyoliona lango la mwenzake.Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kila timu ikifanya mabadiliko wakiwa na matarajio ya kubadilisha mchezo ili wapate matokeo mazuri . Azam ililazimika kumaliza mechi pungufu baada ya mlinda mlango wake Razak Abarola kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mchezaji wa Kagera Sugar nje kidogo ya eneo la hatari. | 4 |
Na KULWA MZEE -DAR ES SALAAM MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuonya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) kwa kutokufika mahakamani mara mbili. Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa alitoa onyo hilo baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kudai kesi ilipangwa kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa upande wa mashtaka lakini mshtakiwa hakuwapo. “Ni rai ya upande wa Jamhuri kwamba mahakama iukumbushe upande wa utetezi kuwa mshtakiwa Lissu ni wakili mzoefu na kwamba utaratibu wa kuomba udhuru mahakamani unafahamika na uzingatiwe,” alidai. Hakimu Mwambapa alisema hiyo ni mara ya pili kwa Lissu kutokufika mahakamani kuhudhuria kesi yake hiyo ambako mara ya kwanza ilikuwa ni Julai 10, 2017 na jana. Wakili wa utetezi, Jeremiah Mtobesya alidai imetokea bahati mbaya lakini Hakimu Mwambapa alimueleza kuwa bahati mbaya mfululizo haiwezekani, hivyo akatoa onyo la mwisho. Jamhuri iliomba kesi hiyo ipangwe tarehe ya karibu kwa ajili ya kusikilizwa na mahakama ilikubali na kupanga iendelee kwa kusikilizwa Agosti 22 mwaka huu. Lissu anakabiliwa na kesi ya uchochezi akidaiwa akiwa katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alitoa kauli za uchochezi kuwa: “Mamlaka ya Serikali mbovu ni ya udikteta uchwara inahitaji kupingwa na kila Mtanzania kwa nguvu zote. “Huyu diktekta uchwara lazima apingwe kila sehemu. Kama uongozi utafanywa na utawala wa kijinga nchi inaingia ndani ya giza nene”. Wakati huohuo, kesi inayomkabili Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, ya kutumia lugha ya matusi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli imeahirishwa hadi Septemba 12,2017 kwa sababu Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa anayesikiliza kesi hiyo hakuwapo. | 3 |
WAKATI sheria ikikataza utoaji mimba holela, imeripotiwa kuwa jumla ya mimba 405,000 zinatolewa nchini kila mwaka huku asilimia 40 kati ya hizo ikitolewa katika mazingira yasiyo salama.Kwa mujibu wa ripoti ya utafiti ya mwaka 2016 iliyotolewa na Taasisi ya Guttmatcher ya Marekani kwa kushirikiana na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Chama cha Madaktari Bingwa wa Uzazi na Magonjwa ya Wanawake Tanzania (Agota), kila mwaka wanawake wa Tanzania milioni moja hupata mimba zisizotarajiwa, asilimia 40 huishia kwenye utoaji wa mimba usio salama. Kati ya hao waliotoa mimba, kinamama 166,000 walipata madhara yaliyotokana na utoaji mimba, wakati 66,000 walitibiwa na 100,000 hawakutibiwa.Pia kuna tofauti za kitakwimu baina ya kanda na kanda. Ripoti ya waratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto Tanzania Bara ya Januari hadi Desemba, 2018 na Ripoti ya Makazi, Idadi ya Watu na Afya (DHS), zinaonesha Mkoa wa Mwanza unaongoza kwa utoaji mimba usio salama ukifuatiwa na Mara. Wajawazito 51 kati ya 1,000 hufanya utoaji mimba usio salama katika Kanda ya Ziwa, wakati 47 kati ya 1,000 ni katika Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, na Zanzibar inashika nafasi ya chini kabisa kwa wajawazito 11 kati ya 1,000.Wastani wa kitaifa ni wajawazito 36 kati ya 1,000. Kwa mujibu wa tafiti hizo ukijumlisha mimba zote zilizotarajiwa na zisizotarajiwa, ni asilimia 3.6 pekee ndio hutoa mimba. Wakati kwa mimba zisizotarajiwa ni asilimia 39. Takwimu hizo pia zinaonesha asilimia 60 hupata matatizo yanayotokana na utoaji mimba, lakini hawapati huduma ya matibabu wanayohitaji kwa wakati mwafaka na hivyo hupata matatizo ya ama kutolewa kizazi, kupoteza maisha au kuziba kwa mirija ya uzazi na matatizo mengine yatokanayo na utoaji mimba usio salama.Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, Anna Temba akizungumza na gazeti hili alisema ili kupunguza vifo vitokanavyo na utoaji mimba usio salama na madhara yake, ipo haja vipengele vinavyohusu haki ya afya ya uzazi vilivyopo kwenye mkataba wa nyongeza ya Afrika kuingizwa kwenye sheria za nchini. “Tanzania ni kati ya nchi zenye uwiano wa juu wa vifo vya wajawazito duniani 410 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa wakiwa hai, na utoaji mimba usio salama ni moja kati ya sababu zinazoongoza,” alisema Temba.Alisema utoaji mimba usio salama unachangia zaidi ya theluthi moja ya wanaolazwa hospitalini kutokana na matatizo yanayohusu mimba na takribani robo moja ya vifo vya uzazi. Akizungumzia takwimu hizo, Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile alisema kwa mujibu wa sheria za Tanzania, utoaji mimba ni haramu na kuwa suala la utungwaji mimba si dharura, kwa sababu hupangwa na wahusika.“Mhusika anapofanya kile kitendo anajua matokeo yake ni nini, ingawa kuna wengine hawafahamu, lakini kutokujua haina maana kuwa ndio uvunje sheria, sheria ipo pale pale. Serikali inatambua mtoto ni yule wa umri chini ya miaka 18 na akifanya tendo la ndoa yule aliyefanya naye atakuwa ameingia matatani maana atakuwa kama amembaka, ingawa kuna changamoto ya sheria ya ndoa inayoruhusu mtu kuolewa chini ya miaka 18,” alisema Dk Ndugulile. | 3 |
Mwandishi Wetu -Singida BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 katika wilaya kadhaa nchini. Misaada iliyotolewa na benki hiyo inayoongoza kwa kutengeneza faida kati ya benki zote zinazofanya biashara humu nchini ndani ya miezi mitano mwaka huu, inahusisha vifaa vya ujenzi, madawati na vifaa vingine vinavyowezesha ukamilishaji wa miradi ya afya,elimu na usalama wa raia. Benki ya NMB imeshatoa msaada wa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa mikoa ya Kanda ya Kati. Akifafanua kuhusu misaada hiyo wakati akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani ingida, Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi, alibainisha kuwa misaada hiyo ya zaidi ya Sh milioni 200 iliyotolewa imelenga sekta ya elimu, afya na majanga kwa mikoa mitatu ya Kanda ya kati. Akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, MkoaniSingida, katika shule ya Sekondari ya New Kiomboi, Mlozi alisema fedha hizo zilizotolewa na NMB zimetumika kununua madawati, viti vya shule za sekondari,vitanda na vifaa tiba kwenye sekta ya afya. Aidha, alisema lengo la misaada hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali. Pia alisema misaada hiyo imekabidhiwa kwa baadhi ya shule, zahanati, hospitali katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Pia NMB walikabidhi madawati 250 na vitanda 80 vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 29.5 kwa baadhi ya shule za Wilaya ya Iramba mkoani humo. Katika hatua nyingine, Benki hiyo imevipatia kituo cha Polisi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro pamoja na shule ya msingi Msowelo mabati 160 yenye thamani ya Sh5 milioni kwa ajili ya kuezekea maboma. NMB iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni mpango wa kuzipunguza baadhi ya changamoto kwa taasisi za serikali hapa nchini, Meneja wa NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus, alisema na kubainisha kuwa msaada huo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ili kusaidia kuinua miradi ya maendeleo. Baraka alisema kuwa kati ya mabati hayo, kituo cha polisi wilaya kimepa tamabati 80 huku shule ya msingi Msowelo nayo ikipata mabati 80. | 5 |
BINGWA mtetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara na wawakilishi wa kimataifa Simba leo wana kazi nzito ya kusaka ushindi katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya robo fainali dhidi ya TP Mazembe ya Congo.Kitendo cha kutinga hatua hiyo ni historia nyingine mpya baada ya mara ya mwisho kufanya hivyo mwaka 2003. Kipindi hicho kutinga hatua ya makundi ilikuwa ndio robo fainali tofauti na sasa mambo mengi yamebadilika kwenye michuano hiyo. Sasa wawakilishi hao wanatamani mafanikio zaidi na nia yao ni kucheza fainali za michuano hiyo. Wekundu hao wa Msimbazi waliwahi kufika hatua hiyo miaka 26 iliyopita mwaka 1993 na tangu hapo uwakilishi wao kwenye michuano ya kimataifa haukuwa wa kuridhisha.Bila shaka kutokana na ubora walionao sasa chini ya mwekezaji wao Mohamed Dewji anayependa mafanikio, kila kitu kinawezekana lakini mtihani walionao ni kuwatoa TP Mazembe. Simba ilibezwa kufika mbali ikadhihirisha mbele ya mashabiki wake na watanzania kwa ujumla kuwa inaweza. Ikahakikisha maadui zake wote hawatambi nyumbani kwake. Ili kuwadhibiti kwa kutumia uwanja wa nyumbani Al Ahly ya Misri anayeogopwa Afrika kwa ubora lakini kwenye uwanja wa Taifa alifungwa bao 1-0, ikampiga AS Vita ya Congo aliyefanya vizuri Kombe la Shirikisho Afrika msimu uliopita kwa kufika fainali, mabao 2-1, JS Saoura ya Algeria.Hiyo ilikuwa ni harakati za makundi lakini leo wapo katika hatua ya robo fainali hatua ngumu kwa vile ni mtoano. Simba inatakiwa kuendeleza ule moyo wa kushinda nyumbani ila ni muhimu kwao kubadilika kwa kushinda mabao mengi zaidi na kutowapa nafasi wapinzani wao kupata bao la ugenini. Kuna makosa yalifanyika kwa wekundu hao katika mechi tofauti kuanzia hatua ya awali walizocheza nyumbani kwa kuruhusu wapinzani kupata mabao ya ugenini. Dhidi ya Mbabane walishinda 4-1, dhidi ya Nkana 3-1 na dhidi ya Vita 2-1 jambo ambalo ni hatari kwao hasa katika hatua hii waliyofikia sasa ambapo umakini unahitajika.Kingine wamekuwa wakiwadharau Mazembe na kusema msimu huu eti sio bora kama miaka mingine. Kama wangekuwa sio bora wasingefika hatua hii muhimu hivyo, wakiwadharau wanaweza kuwaadhibu kwasababu ni timu yenye uzoefu mkubwa na ina wachezaji wengi wazuri. Mazembe sio mara ya kwanza kuja kucheza katika ardhi ya Tanzania, wanaujua vizuri uwanja wa taifa, Dar es Salaam. Waliwahi kucheza nao mwaka 2011 katika mchezo wa pili hatua ya makundi kwenye uwanja huo Mazembe ikashinda 3-2 na ule wa kwanza uliochezwa kwao ikashinda 3-1.Kwa maana nyingine, mechi hii ni wakati sahihi kwa Simba kulipa kisasi kwa Mazembe. Timu hiyo ya Lubumbashi, Congo tayari itakuwa imeshawasoma wapinzani wake kwa kujua kuwa kumbe inakuwa wakali hasa kwenye uwanja wa nyumbani, wanaweza kuja na mbinu zao nyingine kuwadhibiti wekundu hao. Udhaifu uliopo kwa Simba ni kushindwa kumudu michezo ya ugenini.Takwimu za hatua ya makundi katika michezo iliyopita inaonyesha hawakupata bao hata moja katika michezo mitatu tena wakiruhusu kufungwa mabao mengi. Ukitizama kule Misri ilifungwa 5-0 dhidi ya Al Ahly, kule Congo ikafungwa 5-0 dhidi ya Vita na kule Algeria ilifungwa 3-0 dhidi ya JS Saoura. Kutokana na udhaifu huo, hawana budi kubadilika kama wanataka kusonga mbele kwa sababu huenda Mazembe wakaja kutafuta sare kisha wakaona wanaweza kumaliza mchezo wakiwa kwao. Ni ukweli usiopingika kuwa Simba kwa upande wa Tanzania ndio timu tishio kwa sasa kwa sababu kati ya timu 20, ndio pekee imepoteza mchezo mmoja tu katika michezo 22, ikishinda 18 na kupata sare tatu, ikishika nafasi ya tatu kwa pointi 57.Wanapewa uwezekano wa kuwaengua vinara Azam inayoshika nafasi ya pili kwa pointi 62 katika michezo 29 na Yanga inayoongoza katika michezo 29. Sababu wekundu hao wako nyuma michezo saba, ikiwa watashinda watachukua uongozi huo kiulaini. Ukiachana na ubora wao katika ligi, wana kikosi kizuri chenye washambuliaji hatari na tegemeo kama Mnyarwanda Meddie Kagere, Mganda Emmanuel Okwi na Mtanzania John Bocco. Kagere ameifungia timu yake mabao 15 kwenye ligi na michuano hiyo ya kimataifa mabao sita hivyo sio wa kubezwa.Bocco ana mabao 11 na Okwi ana saba kwenye ligi. Simba ikiwa nyumbani bado inajivunia safu bora ya ulinzi baada ya kuruhusu nyavu zake kuguswa mara saba pekee ikiwa ndio timu iliyofungwa mabao machache ingawa kimataifa bado hawako vizuri. Kwa upande wa TP Mazembe sio timu ya kudharauliwa kwani katika ligi ya kwao bado wapo kwenye ubora, wanashika nafasi ya pili kwa pointi 58 nyuma ya AS Vita inayoongoza kwa pointi 65. Timu hiyo ina wachezaji wengi hatari na wenye uzoefu mkubwa kama Tresor Mputu, Kelvin Zatu, Meshaki Elia na Jackson Muleka.Katika michezo yao iliyopita ya hatua ya makundi timu hiyo inaonekana kutokuwa na rekodi nzuri ugenini. Michezo mitatu waliocheza, miwili walipata suluhu dhidi ya Africain, sare ya bao 1-1 dhidi ya Ismaily na kufungwa 3-0 dhidi ya Constatine. Kwa kutizama na takwimu hizo inaonesha kuwa wanaweza kuja na lengo la kutafuta sare wakiamini nyumbani kwao ndio sehemu wanakoweza kupindua matokeo.Mechi zao za marudiano dhidi ya timu hizo walizocheza kwao zinaonesha namna gani matokeo ya nyumbani yaliwabeba. Ilishinda mabao 8-0 dhidi ya Africain, 2-0 dhidi ya Constatine na 2-0 dhidi ya Ismaily. Mchezo wa leo utakuwa mgumu kwa kila mmoja, hasa wekundu hao wanahitaji matokeo mazuri kwenye uwanja wa nyumbani kisha kujipanga na mechi ya marudiano ya ugenini itakayochezwa April 13, mwaka huu. Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems anasema anawaheshimu Mazembe hivyi ataingia kwa tahadhari. “Mazembe nimeifuatilia, ni timu bora na inafanya vizuri kwenye mechi zake, nimewaandaa wachezaji wangu, tutaingia kwa tahadhari kubwa,” anasema. | 4 |
Serikali ya Kenya imetangaza kuongeza mishahara kwa wafanyakazi wa ndani katika miji mikubwa kufi kia Shilingi za Kenya 13,500, ambayo ni sawa na zaidi ya 300,000 za Tanzania .Lakini, kwa upande wake, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) limesema katika kuhakikisha mishahara inapanda katika sekta za umma na binafsi baada ya kukaa kwa zaidi ya miaka mine, wameunda tume maalum kwa ajili ya kuchambua sababu za kutaka mishahara kupanda. Tume hiyo itaangalia namna ya kupanda mishahara kwa wafanyakazi wote, wakiwemo wa ndani, kwa kuongeza kima cha chini cha sasa cha Sh. 100,000. Kwa Kenya, wizara inayoshughulikia masuala ya ajira imetaka waajiri katika miji mikubwa, kuwalipa wafanyakazi wa kazi za ndani kiwango hicho cha mshahara, hasa kwa wanaoishi miji mikubwa ya Nairobi, Mombasa na Kisumu.Aidha, wale wanaoishi katika Manispaa na Halmashauri za miji watawalipa wafanyakazi wao mishahara ya Shilingi za Kenya 12,522, sawa na Shilingi za Tanzania 284,586 au Shilingi za Kenya 600 sawa na 13,600 kwa siku . Hatua hiyo imetokana na wafanyakazi wa ndani kuandamana katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi katika Viwanja vya Uhuru Park. Wafanyakazi watakaonufaika na malipo hayo mapya ni wafanya usafi, wasimamizi wa bustani, waangalizi wa watoto, wasaidizi wa kazi za ndani, walinzi na wahudumu.Marekebisho hayo yamesainiwa na Waziri wa Kazi, Ukur Yattani Desemba 19. Alisema agizo hilo jipya la mishahara, litaongezwa katika posho ya nyumba kwa wafanyakazi. Pia waajiri wanatakiwa kutoa michango katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa mwezi. Rais wa TUCTA, Tumaini Nyamhokya akizungumza na gazeti hili , alieleza mikakati ya shirikisho hilo ni kutaka mishahara katika sekta zote kupanda, tofauti na ilivyo sasa ambapo kima cha chini ni Sh.100,000. “ Kima cha chini hiki kimekaa muda mrefu na sasa tumeunda kamati ya wataalamu kutoka vyuo vikuu na taasisi zisizo za kiserikali, kutusaidia kuangalia hoja zitakazosaidia nia yetu kufanyiwa kazi”alisema Alisema kamati hiyo inatarajia kuwapelekea mapendekezo mwezi ujao ili kuweza kufanyia kazi na kuwasilisha wakati wa Sikukuu ya Mei Mosi na utekelezaji wake ufanyike kuanzia mwezi Julai mwaka huu. | 2 |
AZAM FC jana ilipata ushindi wa kwanza baada ya mechi tano kwa kuwachapa African Lyon Mabao 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa kwenye uwanja wa Uhuru Dar es Salaam jana.Ushindi huo ni wa pili tangu kutimuliwa na aliyekuwa kocha mkuu Hans van Pluijm na msaidizi wake Juma Mwambusi na nafasi zao kushikwa na makocha wa timu za vijana Abdul Mingange na Iddi Cheche.Mabao ya Azam katika mchezo huo yalifungwa na Obrey Chirwa,Mudathir Yahya huku Rolland Msonjo wa Lyon akiwazawadia bao la kujifunga. Lyon walipata bao lao la kufutia machozi kupitia kwa Baraka Jaffari.Ushindi huo umewafanya Azam kuendelea kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi hiyo kwa kufikisha pointi 53 baada ya kucheza michezo 26 wakiwafukuzia vinara Yanga ambao wapo kileleni wakiwa na 61. Lyon wanaendelea kuburuza mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya kufikisha pointi 21 wakishinda michezo minne, kufungwa 15 na kutoka sare michezo tisa.Katika mchezo huo uliokuwa na kasi mwanzo mwisho Azam walikuwa wa kwanza kuandika bao la uongozi dakika ya 6 kupitia kwa Chirwa akipokea pasi kutoka kwa Ramadhan Singano kabla ya Lyon kusawazisha dakika ya 15 kupitia kwa mchezaji wao Jaffari.Timu zote zilianza kipindi cha pili kwaa kufanya mabadiliko ambayo yaliinufaisha zaidi Azam waliopata bao la pili dakika ya 64 kupitia kwa Yahya aliyetumia vyema makosa ya mabeki wa Lyon kushindwa kuondosha mpira eneo la hatari. Dakika ya 89 Lyon walijifunga kupitia mchezaji Msonjo baada kutokea shambulizi la kushtukiza hali iliyofanya mchezaji huyo kukosa umakini na kujichanganya. | 4 |
NA FARAJA MASINDE
ALIYEKUWA PWANI
TAASISI ya Confucius ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), inayofundisha Lugha ya Kichina, imetoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini waliofanya vizuri kwenye masomo ya lugha hiyo.
Akizungumza mwishoni mwa wiki katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi hao iliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Baobab iliyopo Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Profesa Zhang Xiaozhen, alisema wanafunzi walioshiriki wamejitahidi kutokana na mafunzo waliyoyapata.
Alisema walimu waliokuwa wanafundisha masomo ya Kichina wamejitahidi na kuhakikisha kwamba mwanafunzi anaelewa kwa kadiri anavyofundisha lugha hiyo, lengo likiwa ni kuzidi kujenga uhusiano mzuri kati ya Tanzania na China.
“Tulikuwa na walimu wa kutosha ambao waliamua kujitolea kufundisha wanafunzi lugha hiyo na hivyo tunashukuru wanafunzi wamejitahidi kujifunza na kuelewa,” alisema Profesa Zhang.
Alizitaja baadhi ya shule sita zilizoshiriki katika mashindano hayo ya lugha ya Kichina na tamaduni zake, kuwa ni pamoja na Baobao Boys na Girls, St Mathew, King David ya mkoani Mtwara na nyinginezo.
Alisema Taasisi ya Confucius imeandaa zawadi mbalimbali kwa ajili ya washindi hao ambapo ni pamoja na fedha taslimu na cheti ili kutoa hamasa kwa wanafunzi kuzidi kupenda lugha hiyo.
Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari Baobab, Halfan Swai, alisema mwaka huu kumekuwa na mwamko mkubwa wa wanafunzi kujifunza Kichina, ikilinganishwa na miaka iliyopita ambapo wengi walikuwa wanasoma Kifaransa. | 3 |
Rais John Magufuli amemuagiza Msajili wa Hazina Athumani Mbuttuka kuhakikisha kuwa mashirika yote nchini ambayo yamekuwa hayatoi gawio kwa serikali, yanafanya hivyo ifikapo Julai mwaka huu. Ameyasema hayo mapema leo, Jumanne, alipokuwa akizungumza katika hafla ya kupokea gawio la serikali kutoka shirika la simu la TTCL lililofanyika kwenye makao makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam. Rais Magufuli amesema yapo mashirika 253 nchini ambayo huwa hayatoi gawio kwa kigezo cha kuwa yanajiendesha kwa hasara, jambo alilosema wachague kulirekebisha na kuanza kutoa gawio au yafungwe.“Msajili wa Hazina yaandikie haya mashirika yote barua, nataka yaanze kutoa gawio, hakuna haja ya kuwa na mashirika yanayofanya kazi kwa hasara,” aliongeza. Hatahivyo Rais Magufuli amepongeza TTCL kwa kutoa gawio lake la bilioni 2.1/- ikiwa ni mwaka wa pili mfululizo kwa shirika hilo kutoa gawio lake serikalini. Zaidi, ametoa wito kwa ofisi na mashirika ya serikali kuhamasisha watendaji wake kutumia line za simu za TTCL ili kuunga mkono ukuaji wa shirika hilo la serikali, huku akiongeza kuwa japokuwa kwasasa shirika hilo lina wateja milioni 2.2 nchi nzima, idadi hiyo ni ndogo na juhudi zaidi zifanywe kuongeza idadi hiyo. | 3 |
SIMBA jana ilikuwa uwanjani Dar es Salaam ikimenyana na African Lyon kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara katika harakati zake za kutetea taji lake. Katika mechi hiyo Simba ilishinda 2-1.Lakini wakati mabingwa hao watetezi wakipigania taji hilo, kuna kila dalili uongozi wa klabu hiyo kuachana na kocha wake msaidizi Mrundi Masoud Djouma aliyehudumu kwenye klabu hiyo kwa takriban mwaka mmoja.Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba jana, zilidai kuwa uongozi umeamua kuachana nae ili kuinusuru klabu yao iliyo kwenye harakati za kutetea taji lake la Ligi Kuu Bara. Djouma amekuwa kipenzi cha mashabiki wa Simba tangu kuwasili kwake akitokea Rayon Sports ya Rwanda kutokana na mbinu zake uwanjani.“Mpaka leo mchana (jana) uongozi ulishaamua kuachana nae, ilikuwa inasubiriwa akabidhiwe barua tu,” alisema mtoa habari wetu ndani ya Simba.Mapema jana, Kaimu Rais wa SimbaSC, Salim Abdallah ‘Try Again’ alikiri hadharani kwa mara ya kwanza kwamba kocha wake msaidizi Djouma na bosi wake Mbelgiji Patrick Aussems hawana maelewano.Try Again aliviambia vyombo vya habari kwamba kumekuwa na msuguano kwa mabosi hao wa benchi la ufundi, na kwamba hali hiyo ilikuwepo tangu wakati wa Pierre Lechantre aliyeondoka mwishoni mwa msimu uliopita.Kumekuwa na maneno mengi kuhusu Djuma na bosi wake kutokuwa kwenye maelewano na kwamba ndio sababu ya Mrundi huyo kuachwa Dar es Salaam timu hiyo ilipokuwa na mechi za mikoani.Kwa nyakati tofauti viongozi wamekuwa wakikanusha suala hilo, lakini jana kaimu rais alikiri na kuahidi kuja na tamko rasmi kama uongozi.“Nikweli kumekuwa na matatizo ya kujirudiarudia mara kwa mara baina ya Djuma na benchi la ufundi,hasa kwa makocha wakuu akiwemo Pierre Lechantre aliyeondoka,”amesema.Amesema wamekuwa wakifanya jitihada kubwa ya kusuluhisha tatizo hilo lakini hawezi kuzungumza mengi kwa vile watakuja na tamko rasmi baadaye. “Tutakuja na uamuzi mwafaka wa suala hili kwa maslahi mapana ya klabu,” alisema.Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya Simba Boniface Lihamwike amesema uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliopangwa kufanyika Novemba 3 sasa umesogezwa mbele kwa siku moja, hivyo utafanyika Novembe 4 mwaka huu.Alisema, uamuzi wa kusogeza mbele uchaguzi huo umekuja baada ya kubaini Novemba 3 kutakuwa na mechi ya Ligi Kuu kati ya mabingwa hao watetezi dhidi ya JKT Tanzania hivyo ni vyema kutoa nafasi kwa mashabiki kuishuhudia timu yao.Simba inatarajiwa kufanya uchaguzi wa kwanza tangu kubadilisha mfumo na kuingia kwenye hisa ambapo mwekezaji wake Mohamed Dewji amenunua hisa 49 huku 51 zikibaki kwa wanachama. | 4 |
ULAJI wa vyakula visivyokuwa na afya ni moja ya sababu za watu nchini kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza ukiwemo wa moyo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi alisema hayo jana akitoa mada kuhusu afya na mazoezi mkutano wa wahandisi ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Katika mada hiyo, Profesa Janabi alifundisha kuhusu shambulio la moyo, kiharusi, tezi dume, saratani, kukoma hedhi na huduma wanazotoa.Profesa Janabi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo alisema hivi sasa watu wanapenda kula vyakula ambavyo ni hatari kwa afya zao zikiwemo chipsi na baga badala ya kula kwa wingi matunda na mboga za majani. “Dhibitini vyakula mnavyokula ikiwa ni pamoja na kutokula vyakula vyenye mafuta mengi vinavyosababisha mishipa ya moyo kuziba kutokana na mafuta na kusababisha kiharusi. Fanyeni mazoezi ya mara kwa mara,” alisisitiza. Alisema ugonjwa wa moyo ni kati ya magonjwa yanayoua watu wengi wakiwemo watoto ambao wasipopata chanjo muhimu zinazotolewa chini ya umri wa miaka mitano, kuna uwezekano mkubwa watoto kuzaliwa na ugonjwa wa moyo.Alizitaja dalili za shambulio la moyo kuwa ni maumivu kwenye kifua na kwenye mgongo upande wa kulia na kushoto na kuwaomba wanapoona dalili hiyo wawahi kwa daktari. Alizitaja aina za kiharusi kuwa ni mshipa unaopeleka damu katika ubongo kuziba na kushindwa kusambaza damu na mshipa wa damu kupasuka na kumwaga damu katika ubongo ambapo aina hiyo ni ngumu kupona. Kuhusu tezi dume alisema wanaume wenye miaka 50 kwenda juu wako hatarini kupata ugonjwa huo na kuzitaja dalili kuwa ni kwenda haja ndogo mara kwa mara hasa hasa usiku.Kuhusu mwanamke kukoma hedhi, alisema mwanamke aliye katika hali hiyo hawezi kuzaa tena na wengi wao huwa na miaka 50 na zaidi. Alizitaja dalili za kukoma kwa hedhi kuwa ni kupoteza hamu ya kufanya tendo la ndoa, mama kuwa mkali, mwenye hasira, joto la mwili kali. Ili kuhimili hali hiyo, aliwashauri wanawake kufanya mazoezi na kuvaa nguo nyepesi kukinga joto na kuepuka chakula chenye pilipili. | 3 |
Matokeo yanaiweka pabaya Stars kwani sasa ili kufuzu inahitaji ushindi wowote katika mechi ya marudiano itakayochezwa Kigali Rwanda mwishoni mwa wiki ijayo. Timu itakayoshinda mechi hiyo itacheza na mshindi kati ya Sudan Kusini na Uganda ambazo jana zilitoka suluhu mjini Juba.Rwanda ilikuwa ya kwanza kupata bao la kuongoza lililofungwa na Dominique Nshuti katika dakika ya 17. Stars haikuwa inacheza vizuri katika dakika hizo na hivyo kocha wake mkuu, Salum Mayanga alilazimika kufanya mabadiliko ambapo alimtoa Shomari Kapombe aliyeumia na nafasi yake kuchukuliwa na Boniphace Maganga katika dakika ya 18.Mabadiliko hayo kidogo yalizaa matunda na dakika ya 33, Stars ilisawazisha bao hilo kupitia kwa Himid Mao aliyefunga kwa mkwaju wa penalti. Mwamuzi wa mchezo huo, Alier James wa Sudan Kusini aliamuru ipigwe penalti baada ya mchezaji wa Rwanda, Rucogoza Aimambe kunawa shuti lililopigwa na Gadiel Michael.Bao hilo kidogo lilileta uhai kwa Stars ambapo sasa ikawa ikipeleka mashambulizi kwa zamu na wenyeji wake na dakika ya 45 nusura Maganga aipatie bao Stars baada ya kuachia shuti kali lakini kipa wa Rwanda, Ndalishime Erick akapangua.Katika mechi ya jana, Stars ilionekana kuwa dhaifu katika safu ya ushambuliaji iliyokuwa chini ya mshambuliaji mpya wa Simba, John Bocco. Aidha mchezo huo ulitawaliwa na ubabe mwingi hasa katika kipindi cha pili ambapo wachezaji wa pande zote walionekana kutoleana lugha za maudhi.Michuano hiyo ilianziShwa kwa mara ya kwanza mwaka 2009 ilipofanyika Ivory Coast na Stars kuwa miongoni mwa timu za kwanza kufuzu. Tangu wakati huo haijafuzu tena na hivyo inajaribu tena bahati yake katika fainali hizo za mwakani zilizopangwa kufanyika Kenya.Stars: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Gardiel Michael, Nurdin Chona, Salim Mbonde, Erasto Nyoni, Simon Msuva, Himid Mao, John Bocco/ Stahmili Mbonde, Muzamil Yassin, Shiza Kichuya.Rwanda: Ndayishimiye Eric, Marcel Mubumbyi/Latif Bishira, Bizimana Djihad, Dominique Savio Nshuti/Innocent Nshuti, Emmanuel Imanishimwe, Iradukunda Eric, Manzi Thierry, Mico Juastin/Kayumba Soter, Yannick Mukunzi, Nsabimane Aimable na Rucogoza Aimable. | 4 |
MKASA wa mwanafunzi wa Kidato cha Pili kukatiza masomo yake, umechukua sura mpya, baada ya baba wa kambo, Ignas Katula kutuhumiwa kumpa ujauzito.Mtuhumiwa huyo ni Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mirumba Kata ya Kibaoni wilayani Mlele mkoa wa Katavi.Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16, alikuwa akisoma Shule ya Sekondari Kibaoni Kata ya Kibaoni.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Focus Malengo alithibitisha tukio hilo. Amesema mtuhumiwa amekamatwa na yuko Kituo cha Polisi Inyonga, akiendelea kuhojiwa.Kesi hiyo itapelekwa mahakamani baada ya upelelezi wa shauri hilo kukamilika.Akizungumza na HabariLeo kwa njia ya simu, Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibaoni, Alicko Kaminyoge alisema mwanafunzi huyo alibainika kuwa mjamzito baada ya kufanyiwa vipimo katika Kituo cha Afya Usevya.Baba mzazi wa mwanafunzi huyo, amevalia njuga suala hilo na anataka mtuhumiwa afikishwe mahakamani. Alisisitiza kuwa shauri hilo haliwezi kuisha kwa maelewano nje ya Mahakama.“Tulipobaini ni mjamzito, taarifa ilitolewa katika Kituo cha Polisi Kibaoni kwa hatua zaidi za kisheria. Pia taarifa ilitolewa katika Ofisi ya Ofisa Mtendaji Kata Kibaoni”, alisema Kaminyoge.Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Mirumba, wakiwemo majirani, walidai kuwa mtuhumiwa baada ya kubaini mtoto huyo ana ujauzito, alikuwa akihaha kumtoa ujauzito huo ili kuvuruga ushahidi, lakini alikwama.“Hata hivyo jitihada zake hizo ovu ziligonga mwamba baada ya binti yake wa kambo kumkatalia, akidai kuwa anaogopa kufa iwapo atajaribu kutoa,”alisisitiza mtoa taarifa, ambaye ni ndugu wa karibu wa mama mzazi wa binti huyo.Kwa upande wao, mashuhuda kutoka eneo la tukio, walidai kuwa mtuhumiwa huyo amemweka kinyumba mama mzazi wa binti huyo kijijini Mirumba, baada ya kuachana na mumewe.“Msichana huyo aliendelea kuishi na mama yake mzazi kijijini Mirumba huku baba yake mzazi akiishi mjini Mpanda, lakini alipotaarifiwa kuhusu mkasa huu alilazimika kuja kijijini hapa na kumchukua binti na kwenda kuishi naye Mpanda baada ya kuripoti tukio hilo katika Kituo cha Polisi Kibaoni”alisema mtoa taarifa.Ilielezwa kuwa mtuhumiwa huyo, alikamatwa na kushikiliwa kituoni hapo kwa saa kumi na mbili na akaachiwa huru kwa dhamana.Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi Katavi, zimethibitisha kuwa mtuhumiwa huyo juzi alikamatwa na baada ya saa 12 aliachiwa kwa dhamana.“Lakini jana saa saba mchana mtuhumiwa huyo alikamatwa tena kwa mara ya pili na kusafirishwa hadi mji mdogo wa Inyonga ambako yupo mahabusu” alisema Ofisa wa Jeshi la Polisi, ambaye hakutaka majina yake yaandikwe gazetini, kwa kuwa si msemaji.Inadaiwa mtuhumiwa ameshikiliwa na jeshi la polisi kwa mara ya pili, kufuatia shinikizo la baba mzazi wa binti huyo, aliyetishia kufungua mwenyewe mashitaka mahakamani.Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mirumba, Japhet Bundara alikiri kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo ikiwa ni mara ya pili.“Leo (jana) wakazi wa kijiji hiki walijitokeza kwa wingi wakishuhudia mtuhumiwa akipandishwa kwenye gari la polisi lililomsafirisha hadi mji mdogo wa Inyonga ambako yupo mahabusu... Kwa kweli sijui kwa undani mahusiano baina yake mtuhumiwa na mama mzazi wa binti huyo,”alisisitiza.Awali, Jumatatu wiki hii gazeti hili liliripoti habari ya binti huyo aliyetoroka kuozwa, amepachikwa mimba.Alikimbia tukio la kuozwa akiwa na umri wa miaka 12. Lakini, miaka minne baadaye alipachikwa mimba na mtuhumiwa huyo, ambaye ni baba wa kambo.Mwanafunzi huo alikuwa akiishi na wazazi wake katika Kijiji cha China wilayani Nkasi mkoani Rukwa.Mwaka 2013 akiwa darasa la sita Shule ya Msingi kijijini hapo, aligundua baba yake mzazi alikuwa na mpango wa kumuozesha kwa mfugaji mwenye umri mkubwa, hivyo alitoroka kwao.Baada ya kutoroka kwao, alikimbilia Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Nkasi mjini Namanyere, akimtuhumu baba yake mzazi kuwa na mipango ya kumuozesha kwa mfugaji mkoani Shinyanga kwa mahari kati ya ngo’mbe 40 na 50.Ilidaiwa kuwa baba yake, alitumia mbinu ya kumhamishia binti yake huyo mkoani Shinyanga, kwa madai kuwa ataendelea na masomo yake huko, kumbe lengo lake ni kumuoza. | 3 |
MAKABURI yote yaliyopo katikati ya jiji la Dar es Salaam yamejaa, lakini bado watu wanaendelea kuzika.Aidha, imeelezwa kuwa pamoja na serikali kutenga fedha kwa ajili ya kununua maeneo ya kuzikia, wananchi wamekataa kuuza maeneo yao, wakidai kuwa ni uchuro. Mwandishi wa habari hizi alitembelea makaburi kadhaa ya katikati ya jiji kujionea hali halisi na kuzungumza na wakazi wa jirani na maeneo hayo.Mkazi wa Mwananyamala Kwa Kopa, ambaye anaishi karibu na maeneo hayo, alisema kuwa miaka mitano iliyopita, kabla hajahamia maeneo hayo, aliambiwa kuwa makaburi yamejaa, lakini kinachomshangaza watu wanaendelea kuzika katika eneo hilo. “Tangu mimi sijahamia huku nasikia tu makaburi haya yalishajaa lakini cha kushangaza kila siku watu wanazika tu hapa, ukiuliza unaambiwa hili gari la polisi wakimaanisha halijai,” alisema mtu huyo.Vijana wengine ambao wanajishughulisha na uchimbaji wa makaburi kwa nyakati tofauti, walisema kuwa kinachofanyika kwa sasa ni kuchimba katikati ya makaburi yaliyozikwa watu muda mrefu ; au wanachimba tu pengine eneo hilo alishazikwa mtu mwingine. “Haya makaburi mengi hapa mjini yameshajaa tunachofanya kwa sasa ni kuchimba kidogo tu ili mradi tupate eneo la kuhifadhi mwili wa mtu mwingine, ukichimba zaidi unakutana na mifupa ya watu kabisa na sisi tumeshazowea,” alisema kijana huyo, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.Alipotafutwa Mkuu wa Makaburi na Maziko wa Jiji la Dar es Salaam, Nasibu Rashidi alikiri kuwa ni kweli makaburi yote ya katikati ya jiji yamekwishajaa. Alisema kwa jiji la Dar es Salaam, kuna zaidi ya maeneo ya makaburi 140. Alisema makaburi yote yamejaa na hii ni pamoja na makaburi ya serikali, watu binafsi na taasisi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na zile za kidini. “Jambo hili tulishalizungumza muda mrefu makaburi yote ya katikati ya jiji ambapo ndiko watu wengi wanazika yamejaa, hakuna ambako utasema kuna nafasi, kilichobaki tunapachika pachika vinafasi nafasi,” alisema. Katika makaburi hayo, hakuna hata njia tena ya kupita hata kwa watu wanaoenda kuzika, hupita juu ya makaburi mengine au kusimama na kukaa juu yake. Kila ambako kuna kinjia kuna kaburi la mtu mwingine na hii ni katika makaburi ya waslamu au wairisto.Mbali na watu kuzika watu wao, bado kuna miili mingine huzikwa na jiji na hao ni wale ambao hawakutambulika ndugu zao kwenda kuchukua miili yao au wale walioacha maiti hospitali na kuondoka. Nasibu alisema kwa sasa makaburi wanayozika waislamu, wamezuia kujenga kwa sababu wanaweza kuzika zaidi ya mtu mmoja ndani ya kaburi moja. “Uzikaji wa waislamu ni tofauti na wakristo, anazikwa akiwa amelala ubavu kule kwenye mwanandani kwa hiyo eneo linalowekwa alama ya shahidi ndiko ambako kalala mtu, eneo la pembeni yake wanaweza kuchimba tena wakamzika mtu mwingine,” alisema. Alisema ndio maana kila mtu anatakiwa kuweka alama katika kaburi alilozikwa mtu, kuonesha alikolala mtu ili kipande kinachobaki aweze kuzikwa mtu mwingine. Nasibu alisema pia kuwa makaburi hayo, akishazikwa mtu futi kadhaa, anakuja anazikwa mtu mwingine juu yake hivyo halitachimbwa kwa urefu kama la mwanzo kuhofika kukutana na alikozikwa mtu mwingine. Aidha, alisema kuwa kwa makaburi ya wakristo, kuna watu wengine wanaomba wenyewe katika kaburi moja kama alizikwa mzazi mmoja wanaomba kuchimba tena na kumzika mzazi mwingine, hivyo kaburi moja kuzikwa baba na mama na kwamba hawajawahi kupata maombi ya kuzika watu zaidi ya wawili.“Wanaamua kabisa, wanaandika barua kwamba sisi tulimzika marehemu wetu hapa labda baba au mama tunakusudia kumzika mzazi mwingine, kwa hiyo watabomoa kaburi na kuchimba tena, kama mwanzo walichimba futi sita itabidi sasa wachimbe futi tano au nne,” alisema Nasibu. Nasibu alisema kuwa maeneo ambayo kuna nafasi ya kuzika kwa sasa ni yale ya nje ya mji, kama vile makaburi ya Tegeta Kondo, Mbweni, Mivumoni na Mabwepande, lakini watu hawaendi kuzika huko kwa sababu ni mbali. Hata hivyo, alisema kuwa maeneo hayo pia ndani ya muda mfupi, nayo yatakuwa hayatoshi, kwa sababu kama watu wataamua kuhamia kuzika huko, bado yanahitajika maeneo makubwa zaidi. Kwamba maeneo hayo yaliyopo sasa, yalikadiriwa kwa ajili ya watakaoishi maeneo hayo pekee na sio pamoja na watu wengine. Alisema pia kwamba kuna watu walitunza nafasi kwa ajili ya kuzika watu wao wakati huo nafasi zilikuwepo. Makaburi hayo ni yale ya Kinondoni Makaburini na Kinondoni FM. “Ilikuwa kuna nafasi wakati huo, mtu anaona mke wake amekufa amezikwa hapa, anaomba nafasi nyingine tatu kwamba akifa yeye na watoto wake wazikwe hapo kwa kufuatana, analipia kibali basi maeneo hayo kuna ambayo yapo kwaajili yao,” alisema. Aidha, Nasibu alisema kuwa makaburi yakijaa, inatakiwa kuandikwa tangazo, lakini watu wanaendelea kuzika kwa sababu watu hawajawa tayari kuacha kuzika maeneo hayo na kwenda maeneo mengine.“Watu tunapishana uwezo hali ya kipato ni tatizo, watu wanaangalia uwezo wao, kusafirisha mwili kwenda kuzika Tegeta huko anaona hawezi, sanda tu kachangiwa hiyo gari ataitoa wapi, tunatakiwa kuandaa maeneo na pia njia ya kufika watu huko kwa usafiri ambao gharama yake itakua nafuu” alisema Nasibu. Kwa upande wake, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita alisema kuwa ni kweli makaburi yamejaa, hasa yale ya katikati ya jiji na kwamba serikali inatafuta maeneo mengine kwa ajili ya kununua kwa ajili ya kutenga watu kuzikia. “Tangu mwaka juzi, mwaka jana na mwaka huu serikali inatenga shilingi milioni 500 kila mwaka, lakini wana Dar es Salaam wananiangusha wanasema kuwa tunawapelekea uchuro, hawataki kutuuzia maeneo yao,” alisema meya huyo. Mwita aliwaomba wananchi kuelewa umuhimu wa kupatikana maeneo ya kuzikia, hivyo walio na maeneo makubwa wakubali kuuza.Alisema kwa sasa wanazika katika maeneo hayo hayo ambayo tayari yamejaa. Alisema anawashangaa wananchi kwa kushindwa kuachia maeneo yao. “Sasa itabidi tuanze kuomba kila mwenye maiti yake waanze kusafirisha kupeleka mikoani, hii hali sio nzuri kabisa jiji limejaa jamani,” alisisitiza meya huyo. Alipotafutwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alisema kuwa mamlaka ya upangaji ni Manispaa. “Mamlaka ya upangaji kwa mujibu wa sheria ni halmashauri za wilaya, manispaa ndio wanaotengeneza na hivi sasa kuna ‘master plan’ mpya ya Dar es Salaam inatengenezwa,” alisema Waziri Lukuvi. | 3 |
NA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM UAMUZI wa kujitoa uliofanywa na timu ya Taifa ya Chad kwenye mchezo wa marudiano wa kusaka tiketi ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) zinazotarajiwa kufanyika mwakani nchini Gabon, umeondosha matumaini na ndoto za timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kucheza fainali hizo. Chad, katika mchezo wa kwanza uliochezwa Alhamisi iliyopita Uwanja wa Omnisport Idriss Mahamat Ouya, mjini N’djamena, ilikubali kipigo cha bao 1-0. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka la Chad, Moctar Mahamoud, uamuzi huo wa kujitoa ulitokana na kukosa fedha za kutosha za kusafiri kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya Taifa Stars, uliotarajiwa kuchezwa jana Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Kutokana na kujitoa huko, mechi tatu za Chad za kundi G zimefutwa, hata matokeo yake ya michezo iliyopita hayatatambuliwa, hivyo msimamo wa kundi G utakuwa unaongozwa na Misri, yenye alama 4, Nigeria alama 2 na Tanzania alama 1, timu zote zikiwa zimecheza michezo miwili. Muathirika mkubwa wa kujitoa kwa Chad ni Taifa Stars, ambayo ilikuwa na matumaini ya kufuzu kwa fainali hizo na ilionekana kuwa kwenye kiwango bora, ikiwa chini ya kocha mzawa, Charles Mkwasa na nahodha mpya, Mbwana Samatta, anayechezea timu ya K.R.C. Genk ya Ubelgiji. Stars ilianza safari yake kwa kupoteza mchezo dhidi ya Misri kwa kufungwa mabao 3-0, baadaye kutoa sare dhidi ya Nigeria na kuifunga Chad bao 1-0. Baada ya kufikisha alama 4, Stars ilikuwa na kila sababu ya kupambana na kuhakikisha inafanikiwa safari ya kuelekea Gabon, hata kwa nafasi ya pili ambayo ni ya upendeleo. Lakini kwa maamuzi ya Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka la Afrika ‘CAF’ yaliyofanywa Januari 15, 2015 yalidai kwamba kundi lolote litakalosalia na timu tatu kufuatia kujitoa kwa moja kwenye kundi hilo, kinara wa kundi hilo atafuzu moja kwa moja kwenye michuano hiyo. Kwa mujibu wa kanuni za michuano hiyo, kama timu itajitoa kwenye hatua ya makundi, matokeo yake yote yatafutwa. Hivyo, kuna kila dalili kwamba Stars ikajikuta katika wakati mgumu wa kufuzu katika michuano hiyo kwa kuwa itabakiwa na alama moja, huku Misri ambayo ni kinara ina alama 4, Nigeria ikiwa ya pili kwa alama 2. Timu ya Taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’, ambao wamepangwa kuchuana na Misri mjini Alexandria inabidi washinde alama zote ili kumaliza katika nafasi ya kwanza. Wakati huo huo, Misri wanahitaji kushinda mchezo mmoja na kutoka sare mchezo wa pili ili kuweza kujihakikishia safari ya Gabon mwakani. Stars hata ikifunga michezo yote, bado haitakuwa na uhakika wa safari, kwani itakuwa na alama saba ambazo zitakuwa chache ukilinganisha na wapinzani. Licha ya CAF kuitoza faini timu hiyo ya Chad dola za Kimarekani 20,000 na kuwapiga marufuku kushiriki kwenye michuano mwaka 2019, bado maumivu ya Watanzania hayatapona. Matarajio ya Watanzania yalikuwa ni makubwa juu ya kufuzu kwa timu yao, kutokana na kuwa na wachezaji wenye uwezo wa kutandaza soka la kuvutia na wenye kuleta matokeo yoyote wanapokuwa uwanjani. Zaidi ya yote, ndoto na matarajio hayo tayari yameshapotea kwenye vichwa vya Watanzania, hivyo kujikuta wakiendelea kusubiri huenda michuano ya mwaka 2019 Stars ikawa na bahati, lakini Chad imevuruga ndoto ya Watanzania. | 4 |
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema madaktari wote waliosoma kwa fedha za serikali watapangiwa vituo vya kazi.Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk Faustine Ndugulile alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Nanyamba, Abdalah Chikota (CCM). Katika swali lake lake, Chikota alitaka kujua mpango wa muda mfupi wa serikali wa kupeleka madaktari bingwa katika Hospitali ya Mkoa ya Ligula (Mtwara).Alisema kwa sasa wapo madaktari ambao wanasoma katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) na kuwa mara watakapomaliza masomo yao watapangwa na serikali kule ambako kuna mahitaji ya madaktari hao.Dk Ndugulile alisema katika wakati huu wa mpito wakiwa wanasubiri kupeleka madaktari hao Serikali pamoja na Mfuko wa Bima ya Afya NHIF wamekuwa wakiweka kambi mabalimbali wakiwa na madaktari bingwa ili kutoa huduma za kibingwa. Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Mtwara Mjini, Hawa Ghasia (CCM), Dk Ndugulile alisema wizara imefanya tathimini ya mahitaji ya madaktari bingwa na fani zao katika Hospitali zote za mikoa, Kanda maalumu na Hospitali ya Taifa Muhimbili.Alisema tathmini hiyo itawezesha utekelezaji wa uamuzi wa kuwapanga upya madaktari bingwa kwa uwiano kulingana na mahitaji ya kila hospitali hizo. “Lengo ni kuwa kila hospitali hizi zinakuwa na madaktari bingwa wa fani nane. Fani hizo ni pamoja na daktari bingwa magonjwa ya uzazi na wanawake , watoto, magonjwa ya ndani, upasuaji, upasuaji wa mifupa, daktari wa huduma za dharura na magonjwa ya ajali,” alisema.Alisema pia madaktari wengine bingwa wanaohitajika katika Hospitali hizo ni pamoja na daktari bingwa wa huduma za usingizi na daktari bingwa wa huduma ya Radiolojia. Kwa mujibu wa Ndugulile katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/18 wizara iliwapeleka madaktari bingwa wa fani za upasuaji wa kawaida na upasuaji wa mifupa 125 katika Chuo Kikuu cha MUHAS. Alisema madaktari hao wanatarajia kumaliza masomo yao katika mwaka wa fedha wa 2020/21. | 3 |
Akizungumza na gazeti hili, Msemaji wa Simba, Haji Manara alisema kikosi chao kilifika Shinyanga usiku na wachezaji wote wapo kwenye hali nzuri.“Hivi ninavyozungumza na wewe timu ipo mazoezini, tayari tumeshafika Shinyanga tangu jana usiku (juzi) wachezaji wote wapo kwenye ari na wameahidi kushinda mechi hii,” alisema Manara.Katika mechi ya mzunguko wa kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba ililala bao 1-0. Ushindi kwenye mechi hiyo ni muhimu kwa timu zote ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kumaliza ligi katika nafasi za juu.Timu hizo zote zinaingia uwanjani zikitoka kwenye matokeo mazuri, Simba ikiifunga Ruvu Shooting mabao 3-0 katika mechi ya mwisho na Kagera Sugar ikiifunga Mtibwa Sugar mabao 2-1 juzi.Timu hizo zipo katika nafasi ya tatu na ya nne kwenye msimamo, Simba ikiwa na pointi 29 na Kagera Sugar pointi 24. Yanga ndio inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 37 ikifuatiwa na bingwa mtetezi, Azam yenye pointi 33.Akizungumzia mechi hiyo, Kocha Msaidizi wa Kagera Sugar, Mrage Kabange alisema timu yake imejiandaa kushinda kama ilivyofanya katika mechi ya kwanza ilipocheza na Simba kwenye Uwanja wa Taifa.“Kama unavyoona ligi ilivyo ngumu, hatusemi kama tunadharau Simba ila tunataka kuendeleza rekodi ya ushindi na hasa ikizingatiwa tupo kwenye nafasi nzuri,” alisema Kabange.“Lengo letu ni kumaliza kwenye nafasi za juu hivyo tunataka kuendelea kushikilia tulipo, tunajua tukifungwa tutapoteza hesabu zetu, kwa hiyo tumejipanga kushinda.”Katika hatua nyingine, timu ya Coastal Union imeanza kuzipigia hesabu pointi tatu muhimu za wapinzani wao, Tanzania Prison ili kuhakikisha wanazichukua wakati watakapokutana kwenye mechi ya Ligi Kuu kesho.Akizungumza jana baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Popatlal jijini Tanga, Ofisa Habari wa Coastal Union, Oscar Assenga alisema kikubwa zaidi wanachojivunia ni kuendelea kuimarika kikosi hicho.Assenga alisema mipango yao mikubwa ni kuiwezesha timu hiyo kupata matokeo mazuri katika mechi zote zilizosalia ikiwemo kuwataka wachezaji kutimiza wajibu wao wa kuipa ushindi timu hiyo.Alisema dhamira yao kubwa ni kupambana kufa na kupona ili kumaliza ligi hiyo wakiwa nafasi tatu za juu kwenye michuano hiyo ambayo msimu huu imeonekana kuwa na upinzani mkubwa. | 4 |
MANCHESTER, ENGLAND KOCHA wa Manchester United, Van Gaal, amesema mipango yake ya kustaafu soka baada ya kumaliza mkataba katika klabu hiyo bado ipo pale pale kwa kuwa alimuahidi mke wake. Van Gaal amesisitiza kuwa hawezi kumuangusha mke wake Truus kwamba akimaliza mkataba wake mwaka 2017 ataachana na soka ili aweze kutulia na familia yake, hata hivyo kocha huyo amesema hana uhakika kama itawezekana kutokana na jinsi anavyopenda mpira. “Ninaamini nitaondoka baada ya kumaliza mkataba wangu, lakini sidhani kama nitakuwa sahihi kwa maamuzi hayo huwezi jua, ila nakumbuka nilimuahidi mke wangu kwamba nikimaliza mkataba wangu na klabu ya United nitastaafu ili niweze kuwa na familia yangu. “Itakuwa ngumu kuvunja ahadi hiyo kwa kuwa nilisema hivyo huku nikiwa na miaka 55 na ikifika mwaka 2017 nitakuwa nimefikisha miaka 65 na nikishindwa kufanya hivyo nitakuwa nimemkosea mke wangu,” alisema Van Gaal. Kwa sasa klabu hiyo inafanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu nchini England ambapo inaongeza katika msimamo wa ligi huku ikiwa na pointi 16 baada ya kucheza michezo saba. Timu hiyo ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri msimu huu katika michuano mbalimbali, kutokana na ubora wa kikosi chake baada ya kocha huyo kufanya usajili mkubwa katika kipindi cha majira ya joto | 4 |
SERIKALI inajiandaa kuwasilisha bungeni muswada wa sheria kuhusu uwekezaji ili kuwe na sheria moja inayosimamia uwekezaji kwa lengo la kuweka mazingira rafiki ya kufanya biashara.Waziri wa Nchi katika Ofi si ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angellah Kairuki amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati anafungua kongamano la wafanyabiashara wanawake lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) lenye lengo la kusikiliza kero za wafanyabiashara wanawake nchini.Amesema, sheria itakayotungwa itapunguza utitiri wa vikwazo vinavyotokana na kutokuwa na mfumo rafiki kwenye uwekezaji.Waziri Kairuki ameyasema, hayo baada ya kusikiliza baadhi ya kero za wafanyabiashara wanawake.Aidha aliwataka wajenge umoja, wajiamini na kufanya kazi kwa bidii ili kuinua vipato vyao pamoja na kujenga uchumi wa nchi.Akielezea dhumuni la kuwakutanisha wafanyabiashara hao, Mwakilishi wa Wanawake Wazalishaji wa Bodi ya TPSF, Fatma Abdallah alisema taasisi hiyo imewakutanisha wanawake ili kuibua fursa mbalimbali za kiuwekezaji, lakini pia kujadili changamoto wanazozipata.Rais wa Sauti ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania (VOWET), Maida Waziri alisema kuwa kuna changamoto kubwa kwa wajasiriamali wanawake hasa kwenye urasimishaji wa biashara zao, lakini ni vyema serikali ikaangalia zaidi sera na sheria zilizo rafiki ili kupunguza hatari ya kuwakatisha tamaa wafanyabiashara.Maida pia aliiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kutoa fursa kwa wajasiriamali kwenye vyuo mbalimbali ili waweze kuelimishwa juu ya mazingira na jinsi ya kuwekeza.“Kuna changamoto ya elimu, lakini TPSF na Taasisi ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) ina jukumu la kutoa mafunzo lakini pia serikali kupitia vyuo mbalimbali vya ufundi na biashara vinaweza kutoa msaada wa bure kwa wafanyabiashara wenye lengo la kuwainua,” alisema Rais huyo.Kwa upande wa Mwakilishi wa Chama cha Wachonga Vinyago cha Tanzania (TANCRAFT), Louise Mushi alieleza kuwa, wajasiriamali wengi wanawake wanakabiliwa na miundombinu ya kufanyia kazi sambamba na mazingira bora ya kufanya biashara kwenye maeneo ya mipaka.Mwakilishi wa Chama cha Wanawake Wachimbaji Madini Tanzania (TAWOMA), Leilla Jumbe alisema kuwa changamoto kubwa inayowakabili wanawake wengi ni mitaji na kwamba inatokana na wanawake wange kutokuwa na mali au ardhi kwa ajili ya kuweka dhamana. | 5 |
JOHANES RESPICHIUS-DAR ES SALAAM CHAMA cha ACT Wazalendo kimetuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Cuba, Raul Castro kutokana na kifo cha kaka yake ambaye aliwahi kuwa Rais wa nchi hiyo, Fidel Castro, kilichotokea juzi nchini humo. Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Katibu wa Kamati ya Nje ya ACT Wazalendo, John Mbozu, ilisema maisha ya Castro hayakuwa manufaa kwa Wacuba pekee bali kwa dunia nzima hasa nchi zinazoendelea. “Alikuwa ni mmoja ya miamba imara ya mapinduzi ya karne ya 20 kupitia mapinduzi ya ujamaa ya Cuba na ameacha alama ya kudumu katika maisha ya WaCuba na darasa maridhawa kwa nchi zinazoendelea kuweka msisitizo juu ya umuhimu wa ujamaa kwa dunia. “Pia licha ya utitiri wa vikwazo kutoka nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani, Cuba iliweza kufuta ujinga kwa asilimia 99 na ni moja ya nchi zenye mfumo bora wa afya hasa kwa kusomesha madaktari wingi zaidi duniani,” alisema Mbozu. Alisema Cuba imekuwa ikitoa msaada wa madaktari kwa nchi za Amerika ya Kusini, Afrika na Asia hadi kuvuka kiwango kilichowekwa na nchi zote za G8 ikiwa na ukuaji wa uchumi unaokwenda sambamba na maendeleo ya watu wengi. Mbonzu alisema Castro alifungamana moja kwa moja na Afrika kwa kusaidia harakati za ukombozi wa bara hilo kutoka katika makucha ya Ukoloni na Ubeberu ambazo zilikuwa na makao makuu yake nchini. “Afrika itamkumbuka Castro kwa mchango mkubwa ambao ambao nchi yake iliutoa katika kufanikisha harakati za kudai uhuru kwenye nchi mbalimbali za barani Afika kama, Afrika ya Kusini, Namibia, Angola, Msumbiji na Kongo,” alisema Mbonzu. Alisema Cuba imepoteza kiongozi wake, Afrika imepoteza rafiki wa kweli, Tanzania imepoteza mshirika katika ukombozi wa Afrika na ACT Wazalendo imepoteza mjamaa mwenzao. | 3 |
AFRICAN Lyon imetamba kuivurugia Yanga itakapokutana nayo leo katika mechi ya Ligi Kuu kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini hapa.Mechi hiyo inachezwa uwanja huo baada ya Lyon kuufanya uwanja wake wa nyumbani hivyo vinara wa ligi Yanga leo watakuwa wageni. Nahodha wa Lyon, Said Ortega aliliambia gazeti hili jana kuwa kikubwa wamejipanga vilivyo kuhakikisha wanapata matokeo katika mchezo huo utakaokuwa na ushindani mkubwa. “Tuko kamili tayari kabisa kuhakikisha tunaifunga Yanga kwani maelekezo yote tuliyopewa na mwalimu tutahakikisha tunayafanyia kazi na kikubwa ni kupambana ili kupata alama tatu kwani nafasi tuliyopo katika ligi sio nzuri na tunahitaji ushindi,” alisema.Ofisa mtendaji mkuu wa African Lyon, Thabit Kandolo alisema wanashukuru kukaribishwa Arusha kwani wamepata mapokezi makubwa pia kupitia ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. “Tumechagua kituo cha Arusha kwa kuwa timu yetu kwa sasa mbali na mpira wa miguu inajihusisha na masuala ya kampeni ya kulinda tembo na Arusha ndio kitovu cha utalii Tanzania, hivyo tuna wajibu mkubwa wa kuhakikisha jamii inapata elimu ya kutosha kuhusiana na ulinzi wa rasilimali,”aliongeza Kandolo.Alisema ujio wao timu hiyo Arusha utarejesha heshima ya soka iliyopotea kwa muda mrefu kwani anaamini hata timu zilizopo ngazi za chini zitapigana kupanda Ligi Kuu. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo aliushukuru uongozi wa timu ya African Lyon kwa maamuzi waliyoyafanya kutumia uwanja wa Sheikh Amri Abeid pamoja na TFF kuwakubalia jambo ambalo litahamasisha soka na wananchi kufika kwa wingi kushuhudia mpabano huo .Alisema kitendo cha kuchagua mkoa wake ni maamuzi ya busara katika kusaidia kutoa hamasa na kama serikali itashirikiana vilivyo kuelekea mchezo huo. “Mchezo huo wa Ligi Kuu utatoa ari kwa timu zetu zilizo katika ligi daraja la kwanza ambazo ni Arusha United na AFC zote zikipambana kuhakikisha zinacheza Ligi Kuu na kama mkoa tumejipanga kuona kuwa msimu ujao tunakuwa na timu daraja la juu,” alisema Gambo. Aliwasihi wapenzi wa soka mkoa wa Arusha na mikoa ya Jirani wafike kwa wingi kushuhudia mtanange huo wa kukata na shoka. | 4 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.