text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
NA JONAS MUSHI MGAHAWA wa Vitabu-Soma umeanza kufanya utafiti wa kuwatambua wasanii wa kike waliosahaulika licha ya kushiriki katika harakati za kupigania uhuru wa Tanzania. Akizungumza mwishoni mwa wiki katika hafla ya kuwakumbuka wanawake walioshiriki kupigania uhuru, Mkurugenzi wa Soma, Demere Kitunga, alisema wapo wanawake wengi waliopigania uhuru kwa njia ya nyimbo na ushairi lakini wamesahaulika, hawajawekwa hata kwenye vitabu vya historia ya ukombozi. “Ushiriki wa wanawake kwenye harakati za kupigania uhuru ni mkubwa kuliko inavyojulikana, wengi wanamfahamu Bibi Titi Mohamed, lakini wapo wanawake waliokuwa wakiimba na kutunga mashairi yaliyowatia ari viongozi katika kudai uhuru hawajulikani. “Tunafanya utafiti kuwapata ambao bado wapo hai ili tupate majina na kazi zao na wale waliofariki tutaweka majina yao katika vitabu vya historia ili mchango wao uweze kuonekana.” Mtafiti wa Soma, Janet Gabone, alisema changamoto wanayopata ni kutokuwepo mahojiano ya mashuhuda kutambua watu hao kwa kuwa wengi wao hawajaacha kazi zao. Naye Balozi wa Ireland nchini, Fionnuala Gilsenan, aliwataka wasanii wa Tanzania waongeze bidii katika harakati zao za kupigania mambo mbalimbali katika jamii kwa kuwa nafasi yao ni kubwa.
1
MRADI wa kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga nchini Tanzania umeshika kasi baada ya Tanzania kuanza utekelezaji katika hatua mbalimbali huku majadiliano ya ndani kwa nchi yakikamilika Januari mwakani.Waziri wa Nishati, Medard Kalemani amesema hayo baada ya kikao cha mawaziri wa sekta zinazosimamia mradi kwa nchi za Uganda na Tanzania kuwa utekelezaji wa mradi huo haujasimama.Mkutano huo wa ngazi ya mawaziri, ulihudhuriwa pia na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu na mawaziri wa Uganda kutoka sekta zinazoshiriki katika mradi walihudhuria.Amesema hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi kwa upande wa Tanzania tayari wamekamilisha utafiti wa kijiolojia na kijiofizikia na sasa wanaendelea na uchimbaji wa mashimo ambamo bomba hilo la mafuta litalazwa.Aidha amesema uchimbaji mashimo umeshafanyika katika mikoa ya Tanga na Manyara na sasa inaendelea katika Mkoa wa Dodoma, wilayani Kondoa.Vilevile alieleza kwamba tathmini zote za mazingira zimekamilika, taratibu za masuala ya fidia na ustawi wa jamii ambapo mradi utapita zimekamilika na hatua inayofuata sasa baada ya majadiliano kukamilika ni ujenzi.Waziri Kalemani alibainisha kuwa mradi haujachelewa kwani unatekelezwa hatua kwa hatua.“Naomba mkawaeleze wananchi wa pande zote kuwa utekelezaji wa mradi huu haujasimama, kimsingi tunaanza kwa nguvu kubwa kuutekeleza ili ukamilike kama tulivyopanga,” alisema na kuongeza kuwa mwaka jana ulisainiwa mkataba, yakapatikana maeneo, kutoa fidia upande wa Tanga, kukamilisha utafiti wa mazingira, kufahamu ukubwa wa bomba, na sasa kuanza kuchimba mashimo ambapo bomba litalazwa.Amesema Januari 17 mwakani utakapofanyika mkutano kama huo nchini Uganda wamekubaliana kukamilisha majadiliano ambayo lazima yake kwa manufaa ya nchi kama kwa upande wa Tanzania, kuainisha kampuni mbalimbali za ndani ili kuzijengea uwezo na kubainisha utaratibu wa namna ya kuzishirikisha ziweze kunufaika na mradi husika.Aidha, amesema ziko jamii za watanzania ambazo zinalengwa zinufaike na mradi husika na kwamba yako mapato yatokanayo na mradi ambayo yanapaswa yaingie kwenye Pato la Taifa, hivyo ni lazima majadiliano yazingatie taratibu zote ili mradi uwe wa manufaa.Waziri Kalemani amesema majadiliano ya pande hizo mbili yalikuwa chini ya Mwenyekiti ambaye ni Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Irene Muloni na walikubaliana kuwa kila nchi ihakikishe inamaliza majadiliano kwa muda uliopangwa.Akieleza hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo kwa Tanzania alisema kwa sasa wamekamilisha maandalizi ya utafiti wa kijiolojia, utafiti wa kijiofizikia na sasa wanaendelea na uchimbaji wa mashimo kwa kwenda katika mikoa mitatu na tayari wamemaliza Tanga, Manyara na sasa Kondoa mjii Dodoma.Amesema hatua za awali za utekelezaji zimeanza kwa kukamilisha tathmini za mazingira, fidia na ustawi wa jamii imekamilika katika mradi utakapopita na kinachofuata ni ujenzi baada ya majadiliano kukamilika.Waziri Kalemani alisema utekelezaji wa mradi uko katika hatua nyingi umeanza kwa kusaini mkataba, kupata maeneo, kufidia kwa upande wa Tanga, utafiti wa mazingira, kubaini ukubwa wa bomba, kuchimba mashimo ambapo bomba litalala hivyo utekelezaji haujachelewa.Waziri Muloni alisema wamekubaliana kuharakisha mchakato wa hatua za maandalizi ili ujenzi ufanyike kwa wakati na kuwanufaisha wananchi wa nchi zote mbili kama ilivyokusudiwa.Alisema mpaka sasa bado hawajakamilisha suala la uwekezaji kifedha, wanaendelea na majadiliano ili kukubaliana na wawekezaji,wanawasiliana na makampuni ili kukamilisha matarajio yao ya kutumia bomba.
5
UPANDE wa mashitaka katika kesi ya kughushi inayomkabili mfanyabiashara, Shabani Hussein maarufu ‘Ndama Mtoto wa Ng’ombe’ katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, umedai upelelezi wa shauri hilo unahusisha nchi mbili za Tanzania na Australia.Wakili wa Serikali, Elia Athanas alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika. Athanas alidai kuna taratibu baina ya nchi ya Tanzania na Australia ambazo zinaendelea kwa ajili ya kukamilisha upelelezi huo. Wakili wa utetezi, Nashon Nkungu alidai upande wa mashitaka haulipi uzito suala la upelelezi kwa sababu tangu kufunguliwa kwa kesi hiyo Mei mwaka jana, haujakamilika.Alidai wanaomba mahakama iangalie kwa jicho la tatu suala hilo kwa kutenda haki na kuuonya upande wa mashitaka kutekeleza jukumu lake katika kesi hiyo na endapo wakishindwa, ufanye kama sheria inavyotaka ya kuondoa mashitaka hayo. Akijibu hoja hiyo, Athanas alidai kuwa kwa upande wa Tanzania tayari upelelezi huo umekamilika na kwamba wanasubiri upande wa pili ambao wana taratibu zao hivyo hawawezi kuwalazimisha. Pia aliwataka wawe wavumilivu kwani sio nia ya upande wa mashitaka kuchelewesha kesi hiyo.Hata hivyo, Hakimu Kasonde aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 21, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Ndama anakabiliwa na mashitaka matano ambapo anadaiwa kuwa Februari 20, 2014 Dar es Salaam, alighushi nyaraka ya kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited iliruhusiwa kusafirisha makasha manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000.00 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.Pia anadaiwa Machi 6, 2014, Dar es Salaam, alighushi kwa kutengeneza hati ya kibali ya Umoja wa Mataifa ofisi ya Dar es Salaam akijaribu kuonesha kilogramu 207 za dhahabu kutoka nchini Congo zinatarajiwa kusafirishwa na kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited, zimesafirishwa bila jinai yoyote wakati akijua si kweli. Ndama yupo nje kwa dhamana.
3
Mkataba huo ulisainiwa Dar es Salaam jana kati ya mamlaka hiyo na Wizara ya Fedha, ambapo, upande wa TRA uliwakilishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa mamlaka hiyo, Bernard Mchomvu na Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, kwa upande wa serikali. Kiasi hicho cha fedha ndicho kilichoainishwa katika bajeti ya mwaka huu.Katika hafla fupi ya kusaini mkataba huo, Waziri Mkuya alisema, "TRA haina budi kuwatengenezea wafanyakazi wake mazingira mazuri yatakayowafanya wajitume kukusanya kodi na kukataa rushwa".Kwa mujibu wake, mazingira mazuri huwaondolea vishawishi wakusanya kodi, hivyo kuwafanya wafanikishe malengo ya serikali, katika ukusanyaji wa mapato. "Hakikisheni mnakusanya mapato kama ilivyopangwa kufikia malengo tuliyojiwekea.Watakaokwenda kinyume na makubaliano haya ni lazima wafahamu kuwa watawajibishwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma,"Mkuya alisema. Kwa upande wake, Mchomvu alimhakikishia Waziri Mkuya kuwa, mamlaka hiyo imejipanga vizuri kuhakikisha lengo la kukusanya kiasi hicho cha fedha linafikiwa na hata kuvukwa.
5
Mwito huo ulitolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng’i Issa wakati wa uzinduzi wa kadi maalumu ya Benki ya Posta (ATM card) kwa ajili ya vikundi vya Vicoba nchini.Kadi hiyo iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam inatazamiwa kuwarahisishia wanachama wa Vicoba pale wanapokuwa wakishughulikia masuala ya kibenki.Juhudi za kuja na wazo hilo ni matunda ya pamoja ya Benki ya Posta Tanzania, Taasisi ya Maendeleo Endelevu ya Vicoba na NEEC. Kwa sasa, mtandao wa Vicoba una vikundi zaidi ya 5,000 katika mikoa 30.“Hii ni hatua muhimu sana,” alisema Issa.Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Posta, Profesa Leticia Rutashobya alisema uzinduzi wa kadi hiyo maalum ya ATM ni ushahidi tosha kuwa benki hiyo imedhamiria kusaidia wajasiriamali hapa nchini.Naye, Mratibu wa masuala ya afya katika taasisi hiyo ya Vicoba, Ikupa Njela alisema kadi hiyo ni ushindi kwa wanachama wa Vicoba pote nchini.“Kadi hii itasaidia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya vikundi hivi katika nchi yetu,” alisema.Hivi karibuni, NEEC ilitangaza kutoa Sh milioni 700 kwa Benki ya Posta Tanzania kama dhamana ya mikopo itakayotolewa na benki hiyo kwa wajasiriamali hapa nchini.Mpango huu uko chini ya Mfuko wa Taifa wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ulioanzishwa mwaka 2008 ambao pamoja na majukumu mengine unatumika kutoa au kudhamini mikopo yenye masharti nafuu kwa wajasiriamali nchini. Mikopo itatolewa kwa riba ya asilimia 11 kwa mwaka.
5
Mwandishi wetu-Mbeya KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), Dk. Edwin Mhede, amewataka wazalishaji wanaotakiwa kutumia stempu za kodi za kielektroniki (Electronic Tax Stamp – ETS) kuendelea kuzitumia kama ilivyoelekezwa na sheria na taratibu za kodi kwa kuwa ina faida kwa wazalishaji wenyewe. Dk. Mhede aliyasema hayo alipotembelea Kiwanda cha Bia mkoani Mbeya ili kujionea namna stempu za kodi za kieletroniki zinazofanya kazi katika kiwanda hicho. Alisema ETS inasaidia kukusanya taarifa sahihi, si kwa matumizi ya kukadiria kodi pekee, bali inamsaidia pia mzalishaji kujua kiasi alichozalisha na kwa muda gani,  lakini pia itamsaidia kuona kama kuna changamoto yoyote ili aifanyie kazi mapema.  “Ujumbe wangu kwa wazalishaji wengine ni kwamba waendelee kutumia stempu za kodi za kielektroniki kama ambavyo tumeelekezwa na sheria na taratibu za kodi, kwa kuwa inasaidia kuongeza ufanisi katika uzalishaji na kuweka taarifa sahihi za uzalishaji,” alisema Dk. Mhede. Alisema katika matumizi ya mifumo, changamoto hazikosekani, lakini ni vema kutumia na kufahamu changamoto zilizopo na kuzifanyia kazi kwa kuwa si vibaya kuboresha mifumo pale ambapo umegundua changamoto katika matumizi ya mfumo huo. Naye Meneja wa kiwanda hicho, Godwin Fabian, alisema kiwanda chao kinaamini ETS ni msaada kwa wazalishaji kwa kuwa inawezesha kugundua bidhaa zisizo halali na zinazoingia sokoni bila kufuata taratibu za uzalishaji na ulipaji kodi. “Ujumbe wangu kwa wazalishaji wengine waone ni kitu kizuri na wasiogope kutumia stempu za kodi za kielektroniki kwa kuwa kama bidhaa zote zitawekwa stempu hizi, itasaidia kufahamu bidhaa zisizo halali zinazoingia sokoni na hivyo mfumo huu utasaidia kukabiliana nazo. Matumizi ya stempu za kielektroniki za kodi kwa bidhaa zinazotozwa ushuru wa bidhaa, yalianzishwa kuchukua nafasi ya matumizi ya stempu za karatasi ambazo matumizi yake yalihusishwa na vitendo vya ukwepaji kodi pamoja na bidhaa bandia kwa kiasi kikubwa. Hii ni mojawapo ya hatua ya Serikali inayolenga kuboresha usimamizi wa kodi nchini. Wanufaika wa mfumo huu ni Serikali, wazalishaji, waagizaji na watumiaji ambapo faida zake ni kulinda mapato ya Serikali kwa kuzuia bidhaa bandia, kumwezesha mtumiaji kutambua bidhaa yenye stempu halali kwa kutumia simu ya mkononi pamoja na kuongeza uhiari wa ulipaji kodi kwa kutengeneza wigo sawa wa ushindani kwa wafanyabiashara wote wanaozalisha na kuingiza bidhaa nchini. Faida nyingine ni kuwezesha ufuatiliaji wa bidhaa kutoka viwandani, mipakani, bohari zilizoruhusiwa, majengo ya kutunzia bidhaa, sokoni hadi kwa mlaji na kuwezesha usimamizi wa bidhaa zinazotengenezwa au zinazoingizwa kutoka nje ya nchi.
3
Hadi dakika ya 30 Yanga ilikuwa inaongoza kwa mabao mawili. Maboa hayo yamefungwa na Papii Tshishimbi kwa penati na Obrey Chirwa.Mabingwa hao watetezi ni wa pili kwenye msimamo wa ligi kuu Tanzania bara wakiwa na pointi 34 na wanahitaji ushindi ili kuwakaribia vinara Simba, ambao wanaongoza wakiwa na pinti 41.Simba kesho watashuka dimbani kucheza na Mwadui FC kwenye Uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga, Majimaji inayofundishwa na Habib Kondo, jana ilifanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kocha huyo akisema kuwa mchezo huo utakuwa na ushindani.“Najua mchezo utakuwa na ushindani kwasababu Yanga itahitaji kushinda kama sisi ambavyo tunahitaji kushinda ili kutoka katika mstari wa timu zinazofanya vibaya,” alisema Habibu Pia Kondo alisema, wachezaji wake wamejiandaa vya kutosha na wana ari ya mchezo na wamemwakikishia kuondoka na pointi tatu.Yanga yenye pointi 34 endapo itashinda bado itaendelea kubaki katika nafasi ya pili, kwani wapinzani wao Azam FC juzi walicheza na kutoka sare na kubaki nafasi ya tatu.Azam ilitoka sare na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba na kufikisha pointi 34 sawa na Yanga lakini wwakitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa. Majimaji ina pointi 14 katika nafasi ya 14 ikiwa na pointi sawa na Kagera Sugar na Mji Njombe, ambazo zipo kwenye nafasi za mwisho.Vinara Simba ambayo itakuwa wageni wa Mwadui FC kwenye Uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga kesho endapo itashinda itaendelea kuweka pengo la pointi saba na mahasimu wake Yanga.
4
    Na MWANDISHI WETU, KUNA msemo usemao mama ndiyo kila kitu katika maisha. Mtoto anapokosa mama huwa mpweke hivyo kujikuta akiishi maisha asiyoyapenda. Upendo wa mama hauwezi kufananishwa na kitu chochote kile, ndiyo maana wazee wanakwambia radhi ya baba inapoteza mawazo wakati ya mama inaua. Ukimdharau mama maisha yako ni lazima yatakuwa ya kubabaisha hapa ulimwenguni. Schamica Stevenson maarufu kwa jina la Mimi (34) ni mwanamke aliyeungua moto mwili mzima lakini anadiriki kumnyonyesha mtoto wake wa pili licha ya uchungu anaoupitia. Mimi anasema anafanya hivyo ili kuwahamasisha wanawake wengine ambao hawaoni umuhimu wa kunyonyesha watoto wao. Mimi aliungua vibaya na moto akiwa na umri wa miaka miwili, nyumbani kwao katika Jimbo la Michigan, nchini Marekani. Alipopata mtoto wa kwanza hakumnyonyesha akihofia majeraha aliyokuwa nao, lakini baada ya kujifungua mtoto wake wa pili aliamua kumpa haki yake ya kunyonya ziwa la mama. ''Nafanya hivi ili wanawake wenzangu wasikate tama iwapo wana matatizo, kama nilivyofanya mimi nikiwa na miaka 20,'' anasema Schamica na kuongeza: ''Kama matiti yanafanya kazi, basi yanastahili kutumika kwa kuwanyonyesha watoto.'' Katika ajali hiyo ya moto uliosababishwa na sufuria ya maji yaliyokuwa yakichemshwa jikoni, Mimi alimpoteza kaka yake ambaye alikuwa na miaka minane. Mimi anasema kuwa mama yao alishindwa kuwaokoa kutokana na chuma zilizokuwa madirishani. Anasema amekuwa akifanyiwa upasuaji wa ngozi mara kwa mara katika maisha yake, hali iliyomfanya awe na wasiwasi wa  kubeba ujauzito, pindi alipofikisha umri wa miaka 20 kutokana na alama alizokuwa nazo tumboni. Mimi, ambaye kwa sasa anafanya kazi ya ukaguzi msimamizi wa afya, anasema mara ya kwanza hakunyonyesha licha ya kwamba alitamani kufanya hivyo. “Nilikuwa mdogo na sikuwa na uvumilivu wa kustahimili maumivu kwa wakati huo. Ila huyu mtoto wangu wa pili niliamua kujaribu kumnyonyesha baada ya kumuona wifi na binamu yangu wakifanya hivyo kwa watoto wao,” anasema Mimi. Anasema alikuwa na maziwa kidogo hivyo ilimlazimu kutumia pampu na sirinji kabla ya kumpa mtoto titi. ''Muuguzi wa unyonyeshaji alinisaidia mno pindi nilipokuwa hospitalini,” anasema. “Nakumbuka muuguzi aliniambia hali hii itakuwa ngumu huku akijaribu kulitoa na kulifinya titi langu. “Nilikamua maziwa baada ya saa tatu na baada ya kula nikiwa bado hospitali, lakini sikuwa napata maziwa mengi,” anasema. Mimi anasema alikuwa akifanyiwa upasuaji wa ngozi kila mwaka huko Cincinnati hadi alipofikisha miaka 17. Licha ya kuwa na alama mwilini, Mimi anatumia picha zake anazonyonyesha kuhamasisha wanawake wengine kujivunia miili yao. “Inanivunja moyo nikisikia mtu anajitoa uhai kutokana na sura zao zilizoathirika na majanga mbalimbali,” anasema na kusisitiza kuwa yeye hajali lolote na kwamba anatembea kila mahali akijilinganisha na mwanamuziki Beyonce au Tamar Braxton. Anaongeza: “Sikupata ujasiri kwa siku moja, lakini najivunia kuwa mjasiri kwa sasa. Kuna wakati nilijihisi mnyonge kwa sababu mimi ni binadamu, lakini narudi na kumshukuru Mungu kwa maisha yangu na watoto wangu ambao niliweza kujifungua na kuwalea.” Makala hii imeandaliwa kwa msaada wa BBC
0
WATANZANIA wameanza kuchangamkia soko la mihogo la tani milioni mbili nchini China, baada ya viwanda zaidi ya vitano vya kuchakata zao hilo kujengwa nchini.Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda amesema mpaka sasa kuna viwanda vitano vya kuchakata zao hilo kwenye mikoa ya Pwani na Tanga, vilivyojengwa na raia wa China.Alisema mkoani Pwani, kuna viwanda viwili na Tanga vitatu. Kakunda alisema viwanda hivyo, vitakuwa vikichakata mihogo wanayoinunua kutoka kwa wakulima na kisha kuisafirisha nje ya nchi.Aliyekuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage aliwahi kulieleza gazeti hili kuwa Tanzania imepata soko la mihogo la tani milioni mbili nchini China. Mwijage alisema soko hilo kama litatumiwa vizuri, litaiingizia Taifa Dola za Marekani milioni 300 sawa na Sh bilioni 691, huku tani moja ya mihogo ikiuzwa kwa Dola za Marekani 150 ambayo ni zaidi ya Sh 300, 000. Alisema uzalishaji wa zao hilo nchini bado uko chini, kwa kuwa ekari moja inatoa tani tatu ikilinganishwa na China ambako ekari moja inatoa tani 50.Alisema kwa Afrika, Nigeria inaongoza kwa kuuza tani milioni 44 za mihogo nchini China kwa mwaka. Katika hilo, Waziri Kakunda alisema ndani ya miaka miwili kuanzia sasa, Tanzania itakuwa na uwezo wa kuuza tani milioni moja za mihogo nchini China. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan- Trade), Edwin Lutageruka alisema tofauti na miaka iliyopita, hivi sasa mwamko wa Watanzania katika kuchangamkia soko hilo la mihogo nchini China, umekuwa mkubwa.Lutageruka alisema kuna kampuni sita za China hapa nchini katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga, zinazonunua mihogo kutoka kwa wakulima na kuichakata kabla ya kusafirishwa nje ya nchi. Alisema Januari mwaka huu walikuwa na kikao na wadau wa zao la muhogo na miongoni mwa mambo waliyojadiliana ni kuanzisha chama cha wadau hao, ambacho alisema kipo kwenye mchakato wa kupata usajili kama mkakati wa kuhakikisha wananchi na Taifa wananufaika na soko hilo la mihogo.Kwa mujibu wa Lutageruka, zao la mhogo linalimwa takribani nchi nzima, lakini hasa katika mikoa ya Pwani ukiwemo Pwani, Mtwara, Lindi, Tanga na Morogoro. Novemba 2017 akihutubia kwenye sherehe za 68 za Siku ya Taifa la China kwenye Ubalozi wa China nchini, aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Susan Kolimba alisema Serikali ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, zilisaini makubaliano yaliyofungua masoko ya China kwa ajili ya mihogo mikavu kutoka Tanzania.Dk Kolimba alisema kupitia makubaliano hayo, kulikuwa na mazungumzo kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Kichina ya Wuxi Goodways International Trade Ltd (WGIT) kwa ajili ya kusafirisha mihogo kutoka Tanzania kwenda China.
3
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) yenye jukumu la kukadiria, kukusanya na kuhasibu mapato ya serikali, ni miongoni mwa taasisi za umma zilizo mstari wa mbele kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa vitendo katika kutekeleza azma ya serikali ya kuleta maendeleo.Serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha miaka mitatu, imefanikiwa kuongeza makusanyo ya mapato kutoka wastani wa Sh bilioni 850 kwa mwezi mwaka 2015 hadi kufikia wastani wa Sh trilioni 1.3 kwa mwezi kwa sasa. TRA imeendelea kuongeza ukusanyaji wa mapato. Mwaka 2015/16 makusanyo yalikuwa Sh trilioni 12.5, mwaka 2016/17 yaliongezeka hadi kufikia Sh trilioni 14.4 na mwaka 2017/18 yaliongezeka hadi Sh trilioni 15.5.Mapato yote yaliyokusanywa kwa miaka mitatu mfululizo ni Sh trilioni 42.4. Taarifa ya makusanyo ya robo ya kwanza ya mwaka huu wa fedha 2018/19 kuanzia Julai hadi Septemba 2018 inaonesha TRA imekusanya Sh trilioni 3.84 ikilinganishwa na Sh trilioni 3.65 zilizokusanywa katika kipindi kama hicho mwaka wa fedha wa 2017/18.Ongezeko hili la ukusanyaji mapato ni hatua kubwa nchini ambalo kwa kiwango kikubwa limechangiwa na kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi na umma kumwelewa Rais hivyo kujitoa kwa dhati kumuunga mkono.Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa pamoja na viongozi wengine wa serikali wamekuwa wakishiriki mapambano dhidi ya ukwepaji kodi unaosababisha upotevu wa mapato ya nchi. Juhudi za Rais Magufuli zimeshuhudiwa akitekeleza kwa vitendo ahadi mbalimbali alizotoa ikiwamo ya wakati akifungua rasmi bunge la 11 mkoani Dodoma; Novemba 20, 2015. Aliahidi kupambana vikali na ukwepaji kodi na upotevu wa mapato ya serikali.Akifungua Bunge hilo, Rais Magufuli aliahidi kupambana na ukwepaji kodi na upotevu wa mapato ya serikali. Katika kipindi cha uongozi, ameongoza na kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari pamoja na kukemea udanganyifu unaofanyika kwenye risiti za kielektroniki (EFDs). Wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Morogoro mpaka Makutupora jijini Dodoma, Rais alisisitiza kuwa kodi husaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini na kuboresha huduma za jamii.“Napenda kuwahimiza Watanzania wote kuendelea kulipa kodi ili kutekeleza miradi ya maendeleo nchini pamoja na kuboresha huduma mbalimbali za kijamii. Pamekuwepo na mtindo, mtu anapokwenda kununua bidhaa anapewa risiti ya bei ndogo badala ya risiti anayotakiwa kupewa.” “Mtoa risiti na mpokeaji wote kwa pamoja wanaiibia serikali na hivyo wanasababisha kuchelewesha maendeleo, ninawaomba Watanzania tuwe wazalendo,” alisema.Licha ya ongezeko la makusanyo, ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Magufuli, TRA imeboresha mifumo yake ya ukusanyaji mapato kumrahisishia mwananchi kulipa kodi stahiki na kwa wakati. Miongoni mwa hatua zilizofanyika ni a uhakiki wa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) kuboresha daftari la walipakodi na kuifanya itumike katika kufanya mawasiliano na TRA hususani katika huduma za kielektroniki.Katika muktadha wa kuhakikisha watu hawakwepi kulipa kodi, TRA imeendelea kudhibiti uingizaji wa bidhaa za magendo nchini kwa kuimarisha doria sehemu za mipakani na mipaka isiyo rasmi ambayo ni maarufu kwa kupitisha bidhaa za magendo. Udhibiti huu unalenga kuhakikisha bidhaa zote zinazoingizwa nchini zinapitia njia rasmi na zinalipiwa kodi na ushuru stahiki kwa mujibu wa sheria, ikiwa pia ni njia mojawapo ya kulinda viwanda vya ndani.Aidha, TRA kupitia Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi imejikita kuhudumia na kuelimisha walipakodi na wadau mbalimbali waelewe umuhimu wa kulipa kodi kwa hiari kwa manufaa yao na taifa kwa jumla. Kupitia idara hiyo, mamlaka imefanikiwa kuongeza uelewa wa masuala ya kodi kwa wananchi. Hivi sasa semina, vyombo vya habari, machapisho, makongamano, tovuti, mitandao ya kijamii pamoja na kituo cha huduma kwa mteja kilichopo ndani ya TRA hutumika zaidi kufikisha ujumbe kwa walipakodi.Mafanikio mengine ni ufunguzi wa vituo vya pamoja vya huduma mipakani. Miongoni mwa vituo hivyo ni kituo cha Rusumo kilichopo mkoani Kagera kilichozinduliwa Aprili, 2016 na Rais Magufuli pamoja na Rais wa Rwanda, Paul Kagame. Kituo kingine ni cha Mtukula kilichopo mkoani Kagera kilichozinduliwa na Rais John Magufuli na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni Novemba, 2017.Vituo vingine ni Holili kilichopo mkoani Kilimanjaro na Tunduma cha mkoani Songwe. Vituo hivi kwa pamoja husaidia kuharakisha utoaji wa huduma mipakani, kuokoa muda wa kushughulikia mizigo na abiria, kukuza biashara na hatimaye kuongeza ukusanyaji wa mapato baina ya nchi zinazopakana. Sambamba na hayo, serikali imeendelea kuwajali na kuimarisha uhusiano na wafanyabiashara nchini. Kwa kipindi cha miezi sita kuanzia Julai mosi hadi 31 Desemba mwaka huu, serikali TRA imetoa msamaha maalumu wa riba na adhabu katika malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia 100 na mwisho wa kuwasilisha maombi ya msamaha huo ni Novemba 30, 2018.Msamaha huo unalenga kutoa unafuu kwa walipakodi wenye mzigo wa malimbikizo ya madeni ya kodi kwa kuwapa fursa ya kulipa kodi ya msingi (principal tax) baada ya kuondoa riba na adhabu kabla ya Juni 30, 2019. Hadi mwishoni mwa Oktoba mwaka huu, TRA ilipokea maombi ya kusamehe riba na adhabu kutoka kwa walipakodi 2,029 yanayofikia Sh bilioni 245.6.Baadhi ya walipakodi hao wameshapewa majibu na wengine wako katika hatua mbalimbali za kushughulikiwa maombi yao. Kuondoa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi ni hatua mojawapo ya kusaidia wafanyabiashara wenye malimbikizo hayo kutokukwepa kulipa kodi, ikiwa ni sehemu ya ahadi ya Rais Magufuli ya kuhakikisha kuwa, mianya ya ukwepaji kodi inadhibitiwa ipasavyo. Pamoja na mafanikio yote haya, TRA imedhamiria kuongeza kasi ya usajili wa walipakodi wapya, kuendelea kutoa huduma na elimu kwa walipakodi, kuendelea kudhibiti biashara za magendo pamoja na wakwepakodi kuhakikisha kuwa kunakuwa na ongezeko la ukusanyaji wa mapato yatakayoiwezesha nchi yetu kufikia uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo mwaka 2025.
3
Na Mwandishi Wetu Mfanyabiashara na mmiliki wa mabasi ya Super Sami, Samson Josiah maarufu Super Sami, atazikwa leo Alhamisi Machi 16, nyumbani kwao wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza saa tisa alasiri baada ya uchunguzi wa kitatibu kukamilika. Akizungumza na Mtanzania Digital leo kaka wa marehemu Amini Sambo amesema atazikwa leo Magu Mjini baada ya kusafirishwa kutoka Musoma ambako mwili wake ulipelekwa kwa ajili ya uchunguzi. Mfanyabishara huyo anadaiwa kutoweka Februari 27, mwaka huu nyumbani kwake eneo la Mwananchi-Buzuruga Kata ya Mahina Wilaya ya Nyamagana Jijini Mwanza na gari lake kupatikana Machi 9, mwaka huu likiwa limeteketea kwa moto kando ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kisha mwili wake kupatikana Machi 14, mwaka huu ukiwa umefungwa kwenye viroba ndani ya Mto Rubana. Ilielezwa kuwa siku aliyotoweka Super Sami alikuwa katika harakati za ununuzi wa nyumba katika Mji Mdogo wa Ramadi Wilaya ya Busega Mkoa wa Simiyu eneo ambalo ni njia kuu ya kwenda mkoani Mara na jirani na lango la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.   Mpaka sasa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara limetangaza kuwashikilia watu watano ambao majina yao hayajatajwa kwa uchunguzi wa kifo cha Super Sami, huku habari za ndani ya zikieleza kuwa wanaoshikiliwa ni pamoja na watu waliohusika na kuwasiliana naye siku ya tukio ikiwa ni pamoja na kutaka kuuziana naye nyumba hiyo.
3
Mwijage aliyasema hayo jana Dar es Salaam wakati alipofanya ziara katika viwanda vinne ikiwemo kiwanda cha nondo cha Kamal na viwanda vitatu vya vilainishi mitambo.Alisema kutekelezwa kwa sheria hiyo kutasaidia ukuaji wa viwanda vingi ambavyo kwa sasa vipo katika hali mbaya baada ya bidhaa zilizo chini ya viwango kuingizwa nchini na kuuzwa kwa bei ya chini.“Sheria hii naona haifanyi kazi hapa nchini na hatuwezi kuendelea kuangalia viwanda vyetu vinakufa wakati sheria tunayo wenyewe lazima ifanye kazi vijana wetu wapate ajira na kuongeza pato la taifa,” alisema Mwijage.Aidha, Mwijage akiwa katika kiwanda cha nondo cha Kamal, alisema viwanda vinapaswa kuzalisha bidhaa bora zitakazoendana na soko kwa kufanya hivyo kutasaidia kukuza uchumi.Akiwa katika kiwanda hicho, alikutana na malalamiko ya soko la nondo lililoathirika na uingizaji wa nondo kutoka nje ambazo huuzwa kwa bei ya chini.“Tunasaidia serikali vitu vingi ikiwemo kulipa kodi, tunaomba mtusaidie tumetengeneza bidhaa kwa miaka miwili hatuna soko inafikia hata vijana wetu wanasimamishwa kazi hakuna mishahara,” alisema John Nekemwene kwa niaba ya Mkurugenzi wa kiwanda hicho.Akiwa katika viwanda vya vilainishi, waziri aliwataka waingizaji wa vilainishi nchini kuhakikisha wanapata kibali kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ambacho kinaeleza ni bidhaa gani analeta na ina ubora wa namna gani.Mwijage aliitaka TBS kusimamia agizo hilo na ifikapo Mei mosi wafanyabiashara hao wawe wameshatoa taarifa tofauti na hapo hatatakiwa kukagua biashara ya mtu ambaye hakutoa taarifa.“Nimetoa muda huo na Mei hatutampokea mtu na bidhaa yake. TBS msimamie hili na atakayeleta bidhaa yake awe ana kibali chenye taarifa tofauti na hapo msihusike kukagua biashara yake,” aliongeza.
5
Na ASHA BANI BENKI ya Biashara Afrika (CBA) Tanzania Limited imeungana na Serikali katika kuhakikisha inapambana na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona. Katika hilo, CBA imetoa msaada wa matanki ya kuwekea maji yenye thamani ya Sh milioni 10 kwa hospitali kubwa nne za jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuunga mkono mapambano ya ugonjwa huo. Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa Hospitali ya Mwananyamala, Amana, Lugalo na Sinza, Ofisa Mtendaji Mkuu wa CBA, Gift Shoko alisema hiyo ni hatua ya awali ya kuunga mkono Serikali na jamii. “Lengo la kufanya hivi ni kuonyesha jinsi gani benki inaendelea kujali jamii na watu wake, inajali wateja na pia kushirikiana na Serikali kwani pasipo kujilinda ugonjwa huu ni hatari pia,” alisema Shoko. Aliongeza kuwa mchango huo ni sehemu ya hatua zinazochukuliwa na CBA katika kuunga mkono jitihada za Serikali kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa Covid–19 nchini. “CBA imeweka nia thabiti ya kusaidia hospitali kwa kugawa vifaa vinavyohitajika kutakasia mikono ili watu waweze kunawa mikono kama njia muhimu ya kuzuia maambukizi. “Mara baada ya kuona ongezeko la mahitaji ya kunawa mikono, CBA ilianza mchakato wa kuandaa matenki ya kuhifadhia maji ili kuwezesha watu kunawa mikono wanapokuwa hospitalini, maeneo ambayo ni muhimu kwa afya ya wakazi wa Dar es Salaam. “Kama tunavyojua, virusi vya corona pia huenea kwa kugusa maeneo yaliyo na maambukizi, hivyo tumehakikisha kuwa matenki hayo yana pedali za miguu ili kuwakinga zaidi watumiaji wa matenki hayo,” alisema Shoko. Alisema CBA inatoa elimu kupitia barua-pepe, ujumbe mfupi wa simu, mabango katika maeneo mbalimbali pamoja na mitandao ya kijamii (Facebook na Twitter) ili kutoa taarifa sahihi kuhusu Covid-19 na jinsi ya kulinda, kuzuia maambukizi na kuchukua hatua mbalimbali. “CBA imeweka msisitizo mkubwa kwenye usalama wa wafanyakazi na wateja wetu kwa kuweka vitakasa mikono katika njia zote za kuingia benki na katika vyumba vyote kwa matumizi ya wateja na wafanyakazi,” alisema Shoko. 
0
SERIKALI imeagiza mashine zaidi ya 60 za kusafi shia fi go kutoka nchini Saudi Arabia zifungwe katika hospitali za rufaa za mikoa ili kuwarahisishia wahitaji wa huduma ya kusafi shwa fi go kuifi kia kirahisi.Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema hayo bungeni jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilolo, Venance Mwamoto (CCM). Mwamoto alihoji kwa nini serikali isiweke mashine za kusafishia figo katika hospitali za rufaa za mkoa kwa sababu tatizo la magonjwa yasioambukiza limeongezeka na mojawapo ni matatizo ya figo.Akijibu swali hilo, Waziri Ummy alikiri kuongezeka kwa magonjwa yasioyoambukiza na ndio maana serikali imeona umuhimu wa kuagiza mashine hizo za figo kutoka Saudi Arabia na kuwa zitakapofika zitafungwa katika hospitali za rufaa za mikoa ambazo itakuwa rahisi kwa wananchi kuzifikia. Hata hivyo, alisema changamoto iliyopo ni kukosekana kwa wataalamu wa mashine hizo na kwamba serikali inazungumza na Serikali ya Suadi Arabia ili ilete watalaamu wake na kuwapeleka katika hospitali kubwa kama vile KCMC, Muhimbili, Bugando ili kuwezesha huduma hiyo.Katika hatua nyingine , Waziri Ummy alisema serikali ilipokea mashine za kufulia Julai mwaka jana na imeanza kuzifunga katika hospitali za rufaa za mikoa. Alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Mariam Kisangi (CCM), aliyebainisha kuwa kuna changamoto ya mashine za kufulia katika hospitali za serikali za Mkoa wa Dar es Salaam na kuhoji kama serikali haioni umuhimu wa kufunga mashine hizo.Awali, akijibu swali la msingi lililoulizwa na Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia (CCM), Waziri Ummy alisema huduma za CT-Scan sasa zinapatikana katika ngazi ya hospitali za rufaa za mikoa na huduma ya MRI zinapatikana katika ngazi ya hospitali za Rufaa za Kanda na Taifa. Mtulia alihoji ni lini serikali itanunua mashine ya CT-Scan na MRI kwa ajili ya hospitali ya rufaa ya Mwananyamala ili kupunguza msongamano katika hospitali ya Muhimbili na kuongeza ufanisi katika hospitali hiyo.
3
DAVAO, PHILIPPINES KATIKA mlolongo wa kauli zake tata kuhusu mashambulizi ya kingono, Rais Rodrigo Duterte ameripotiwa akisema atawapongeza wabakaji wakitenda jinai itakayowahukumu kifo. Akizungumza na wanadiplomasia wa Ufilipino Ijumaa iliyopita katika mji wa nyumbani wa Davao, ambako alihudumu kama meya kwa zaidi ya miongo miwili, Duterte alizungumzia masuala ya uhalifu unaotokana na mihadarati, ikiwamo ubakaji. “Kile nisichopenda ni watoto kubakwa. Mnaweza kubaka pengine mrembo wa Miss Universe. Hapo naweza kukupongeza kwa ujasiri wa kumbaka mtu ukifahamu kuwa utaishia kunyongwa,” Duterte anadaiwa kusema. Duterte  (72), aliukwaa urais mwishoni mwa Juni 2016, na kipindi kisichozidi mwaka mmoja baadaye, alilaaniwa duniani kwa vita dhidi ya unga, ambayo imesababisha maelfu ya mauaji na ukiukaji wa haki za binadamu. Wakati akiendesha kampeni za urais Aprili 2016, Duterte alitoa kauli za kutisha kuhusu mmisionari wa Australia, ambaye alibakwa na kundi la watu na kuuawa wakati wa uasi gerezani mwaka 1989 mjini Davao, wakati akiwa meya. “Niliona uso wake na kujiwa na wazo: Wapumbavu, wamembaka kwa zamu, walipanga foleni. Nilikasirika kuwa alibakwa, lakini alikuwa mrembo. Nilidhani kama meya nilipaswa kuwa wa kwanza,” alisema. Baadaye aliwaambia wakosoaji wake maneno hayo hayakuwa utani na aligoma kuomba radhi. Mei mwaka huu, Rais Duterte aliwaambia askari wake angewaruhusu kubaka wanawake watatu kila mmoja. “Fanyeni kazi yenu. Mengine niachieni. Nitaenda jela kwa ajili yenu. Iwapo mtabaka watatu, nitaikubali,” alisema. Na wakati binti yake mwenyewe alipotangaza kuwa mwathirika wa ubakaji, Rais Duterte anaripotiwa kupuuza madai yake akimwita ‘malkia wa maigizo.’ Tangu aukwae urais, ametoa kila aina ya kauli tata kuanzia kumtusi Rais Barack Obama hadi kudai ameua wahalifu kwa mkono wake na kuwala nyama.
2
Ujenzi wa Kituo cha Afya Msanzi mkoani Rukwa, haujaanza kwa miezi nane sasa, kutokana mvutano uliopo kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Joachim Wangabo na Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Julieth Binyura.Kwa sasa kila mmoja ana na eneo lake, ambalo anataka kituo hicho kijengwe, huku Mbunge wa Jimbo la Kalambo ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Josephat Kandege anapendekeza eneo la Samazi, ilipo Zahanati ya Samazi.Akizungumzia suala hilo, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) anayeshughulikia Afya, Dk Dorothy Gwajima ameeleza kuwa anasikitishwa na kuchelewa kuanza kwa ujenzi wa mradi huo kwa miezi nane sasa.Hivyo, Dk Gwajima amempa siku saba Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, Msongela Palela , ahakikishe ujenzi wa Kituo cha Afya Samazi unaanza mara moja.Alionya kuwa vinginevyo Sh milioni 400 zilizotolewa na Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo, zitahamishiwa akaunti ya Kata ya Msanzi mwambao mwa Ziwa Tanganyika na ujenzi kusimamiwa na kamati ya afya ya kata hiyo.“Serikali Kuu imeshatoa shilingi milioni 400 kwa ujenzi wa Kituo cha Afya Samazi tangu Mei mwaka jana. Fedha zipo ila mnavutanavutana, pia shilingi bilioni 1.5 zimeshatolewa kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kalambo, ambako nako taarifa nilizonazo zimetumika zote na kazi haijakamilika huku ikidaiwa nyongeza ya shilingi milioni 701” alisema Gwajima.Alisisitiza kuwa “Msimamo na maelekezo ya Wizara, Ofisi ya Rais Tamisemi ni kwamba ujenzi wa Kituo cha Afya ufanyike katika eneo lililopo Zahanati ya Samazi na si vinginevyo. Nampa DED siku saba ujenzi uanze vinginevyo shilingi 400 zilizopo katika akaunti ya DED zitahamishiwa katika akaunti ya Kata ya Msanzi na ujenzi kusimamiwa na Kamati ya Afya ya Kata ya Samazi”.Dk Gwajima alitoa maagizo hayo ya serikali, alipotembelea na kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya Samazi na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Matai, akiwa katika ziara ya siku mbili mkoani Rukwa.Akizungumzia hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Samazi, Bernard Kapesa aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kutokana na mvutano wa wapi kijengwe kituo cha afya, wakazi wa Kata ya Samazi wamelazimika kusafisha maeneo yote matatu.“Mkuu wa Mkoa (Wangabo ) ana eneo lake, tena alikuja na wataalamu wake, tumeshalisafisha, DC (Binyura ) naye hivyo hivyo, tumelisafisha eneo analolitaka na tena tumepasua na barabara ya kufika huko... Mbunge (Kandege) naye pia ana eneo lake, tumeanza kulisafisha kwa kuchimbua mawe... kwa kweli tumechanganyikiwa na kuteseka, kila mmoja ana maelekezo yake,”alieleza Kapesa.Kwa upande wao, wakazi wa Kata ya Samazi walimweleza Dk Gwajima kuwa wao wanapendelea kituo cha afya kijengwe katika eneo ilipo zahanati ya Samazi na si vinginevyo.
3
NA LULU RINGO TIMU iliyopanda daraja kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2018/19, African Lyon leo imemtambulisha kocha na mchezaji wote raia wa Ufaransa kwa lengo la kusaidia timu hiyo ifanye vizuri kwenye ligi hiyo. Kocha huyo mpya anayetambulika kwa jina la Soccoia Lionel na mchezaji anayetambulika kwa jina la Victor Dacosta wote kwa pamoja wameingia mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu hiyo. Kocha huyo aliyewahi kuifundisha AFAD ya Ivory Cost, CIFAS ya Benin na Cotton Spots ya Gabon amesema amejiandaa vizuri kupambana na ligi kuu ya nchini Tanzania na anaimani timu yake itafanya vizuri. Naye Victor Dacosta aliyeonekana kuwa na furaha mno amesema ndoto yake ya muda mrefu ilikuwa ni kucheza Ligi Kuu ya Tanzania. “Naipenda Tanzania tangu nikiwa mdogo ina mazingira mazuri na hali ya hewa nzuri tamaa yangu kwa muda ilikua kucheza Ligi Kuu nchini Tanzania, kwasasa nina furaha sana” Alisema Victor. Naye Meneja wa timu hiyo, Adam Kipatacho amesema timu hiyo imefanya usajili mzuri japo watu wengi wanatizama usajili wa vilabu vyenye majina makubwa tu na kusahau timu zenye majina madogo kama timu yake. “Wengi wanatizama usajili wa timu kubwa, lakini katika timu zilizofanya usajili mzuri basi African Lyon ni mojawapo,” alisisitiza Meneja huyo.
4
KWA mwaka 2017 na 2018 waajiri tisa wamefi kishwa mahakamani kutokana na kukiuka taratibu na sheria za ajira.Hayo yalielezwa jana bungeni na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu, Hadija Nasri (CCM). Katika swali lake, Nasri alitaka kujua serikali ina mikakati gani ya kulinda wafanyakazi kutokana na kuwepo kwa malalamiko mengi juu ya waajiri kwa kutozingatia sheria ya ajira.Pia alitaka kujua nini kauli ya serikali kutokana na kuwepo kwa malalamiko mengi ya waajiriwa kuwalalamikia waajiri lakini hakuna mkakati wowote ambao unafanyika kwa ajili ya kuwatetea. Akijibu, Mavunde alisema serikali imekuwa ikihakikisha waajiri wanafuata sheria na kanuni za ajira na kuwa wale wanaokiukwa wanafikishwa katika vyombo vya sheria.Awali, katika swali la msingi la mbunge wa Viti Maalumu, Munira Khatibu (CCM) alisema kuwa baadhi ya kampuni binafsi zimekuwa zikiwafanyisha kazi watumishi wao zaidi ya muda wa saa za kazi. Mbali na kufanya kazi zaidi ya muda wa kazi wamekuwa hawapewi chakula na kuwalipa kima kidogo cha mshahara. Kutokana na hali hiyo mbunge huyo aliihoji serikali na kutaka kujua serikali ina kauli gani juu ya suala hilo linalowakandamiza wafanyakazi wengi ambao wengi ni vijana.
3
NA OSCAR ASSENGA, TANGA ULIPUAJI wa milio kwenye pikipiki (Exose) maarufu kama jango moshi, umetajwa kuwa miongoni mwa ugaidi mpya unaoitesa jamii ya Watanzania wengi ambao wameshindwa kuishi kwa amani. Kutokana na hali hiyo, Jeshi la Polisi limetakiwa kuona namna ya kudhibiti hali hiyo. Hayo yamesemwa jana na Sheikh wa Msikiti wa Bilal Muslim wa mjini Tanga, Mohamed Mbaraka, wakati wa kikao cha pamoja baina ya viongozi wa dini na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba. Alisema jambo hilo halina tofauti na ugaidi kutokana na kuwa milio hiyo imekuwa ikilipuliwa hadi saa nane usiku watu wakiwa wamelala majumbani mwao. “Ukiangalia ndugu yetu Kamanda wa Polisi, watu wamekuwa wakifikiria ugaidi ni vitendo vibaya, viovu tu, hata suala la ulipuaji wa milipuko kwenye pikipiki maarufu kama jango moshi, nao ni hatari,” alisema. Naye Mchungaji wa Kanisa la Moravian Chumbageni, Ibrahim Nzowa, aliunga mkono hoja hiyo na kusema jambo hilo ni hatari. Naye Kamanda Wakulyamba aliwataka viongozi wa dini kuacha kuwakumbatia watu wachache wanaotumia mianya ya dini kufanya vitendo viovu.  “Viongozi wa dini wana nguvu za Mwenyezi Mungu na kiroho ambazo wanaweza kuzitumia kwa ajili ya kuibadilisha jamii… umoja wenu huu ni muhimu katika masuala ya usalama,” alisema.
3
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza  hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi.  Kwa misingi kama hiyo sisi kama  chombo cha habari  tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk.  Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia.  Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”.  Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi,  Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii.  Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo.  Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge.  viongozi  wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo.
5
Elizabeth Kilindi,Njombe KUTOKANA na agizo la Rais Dk. John Magufuli la kutaka stendi kuu mpya  ya Njombe  kuanza kutumika ifakapo Mei 10,2019 hatimaye stendi hiyo imeanza kazi rasmi. Akizingumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Ruth Msafiri, aliwapongeza wananchi kwa kuitikia wito wa kuhamia katika stendi mpya licha ya kuwepo na shughuli za ujenzi wa stendi hiyo zikiendelea. “Nawapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi.Wengi mmekuja kushuhudia kama kweli stendi imeanza lakini pia kwa wasafiri, wadau wa vyombo vya usafirishaji mwitikio umekuwa mkubwa na hii inaonesha wazi jinsi mlivyokuwa na kiu ya siku nyingi kuitumia stendi hii” alisema Ruth na kuongeza. “Tunamshukuru Rais Magufuli kwani kupitia maelekezo yake  kumefanya stendi hii ianze kufanya kazi, ametusaidia sana katika kutusukuma katika siku hizi za mwishoni  na leo tumetekelza agizo lake stendi imeanza kufanya kazi na wananchi wanafuraha iliyopitiliza”alisema. John Msemwa ni miongoni mwa abiria waliofika kwenye stendi mpya ili kujionea huduma alisema changamoto nyingi kwa sasa zimepungua ukilinganisha na stendi ya awali. “Kwanza stendi ya zamani ilikuwa ndogo sana hii stendi ni kubwa, miundombinu ni mizuri vyoo maji yapo vyoo vizuri, visafi hata ukiangalia huku hakuna matope kama kule kwenye stendi ya mwanzo. Stendi ya awali matope mengi hasa wakati wa mvua hakuna hata sehemu ya kukaa.huku kuna maeneo mengi ya kukaa ikikamilika itakuwa kivutio” alisema Msemwa. Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda, alisema mpaka sasa ujenzi wa stendi hiyo umekamilika kwa asilimia 95 na kuwa shughuli zolizosalia zinatarajia kukamilishwa ndani ya wiki mbili zijazo. “Tunashukuru kwa pongezi kwani haikuwa kazi rahisi, asilimia tano zilizosalia tutazikamilisha ndani ya wiki mbili licha ya mabasi kuanza. Tulikuwa pia na kikao na wahandisi ili kuona ni namna gani kazi zilizosalia tunazikamilisha ndani ya wiki mbili licha ya kuwepo na changamoto ya mvua za mara kwa mara,”alisema Mwenda. Mwenda aliongezea kuwa licha ya kutoa huduma kwa wananchi stendi hiyo pia ni chanzo kikuu cha mapato kwa Halmashauri hiyo na wanataraji kukusanya milioni mia tatu kwa mwaka hayo yakiwa ni makisio ya chini. Mkurugenzi huyo pia aliendelea kuwasisitizia wananchi kuhakikisha kuwa wanafuata utaratibu uliowekwa wa kuchangia gharama ya Sh 200 kwa wale ambao wanaingia stendi pasipokuwa na tiketi ya abiria. Akizungumzia suala wa wajasiriamali wadogo alisema umeandaliwa utaratibu mzuri na punde wataelekezwa utaratibu kwa wajasiriamali hao na amewasisitiza kuhakikisha kuwa wanakuwa na kitambulisho cha wajasiriamali. Mwenda aliwapongeza wananchi kwa mwitikio wao na kusema kuwa ataendelea kutoa tarifa ya mabadiliko yoyote yatakayokuwepo katika stendi hiyo kadri muda unavyozidi kwenda na kwa kadri ya matengenezo yanayoendelea katika stendi hiyo.
3
WATAHINIWA 91,442 wa shule na wa kujitegemea wamesajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha sita (ACSEE) unaoanza leo nchini kote. Aidha, jumla ya shule za sekondari 731, vituo vya watahiniwa wa kujitegemea 229 na vyuo vya ualimu 90, zitatumika kufanyika mitihani hiyo.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani Tanzania (NACTE), Dk Charles Msonde amesema watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 80,305 kati yao wanawake ni 46,224 sawa na asilimia 57.56 na wanawake ni 34,081 sawa na asilimia 42.44.Dk Msonde alisema watahiniwa wenye mahitaji maalumu ni 102 kati yao 67 ni wenye uoni hafifu, 16 wasioona, 18 wenye ulemavu wa kusikia na mlemavu wa akili. “Mwaka 2018 idadi ya watahiniwa wa shule walikuwa 77,222 hivyo kuna ongezeko la watahiniwa 3,083 sawa na asilimia nne kwa mwaka 2019 ukilinganisha na mwaka jana,” alisema Dk Msonde.Alieleza kuwa watahiniwa wa kujitegemea ni 11,117 ambao wanaume ni 7,190 sawa na asilimia 64.68 na wanawake ni 3,927 sawa na asilimia 35.32 huku watahiniwa wa kujitegemea wenye uoni hafifu ni 15 na kwamba waliosajiliwa mwaka jana ni 10,421.Kwa upande wa mtihani wa ualimu, Dk Msonde alisema jumla ya watahiniwa 12,540 wamesajiliwa kufanya mtihani wa kozi za ualimu na kati yao 7,594 ni ngazi ya stashahada na 4,946 ni wa ngazi ya cheti.Kati ya watahiniwa 7,594 wa stashahada waliosajiliwa 5,616 sawa na asilimia 74 ni wanaume na 1,979 sawa na asilimia 26 ni wanawake na kati ya watahiniwa 4,946 waliosajiliwa 2,795 sawa na asilimia 57 no wanaume na 2,151 sawa n asilimia 43 wanawake.Alieleza kuwa mwaka 2018 idadi ya watahiniwa wa ngazi ya ualimu waliosajiliwa walikuwa 7,422 hivyo kuna ongezeko la jumla ya watahiniwa 5,118 sawa na asilimia 41 kwa mwaka 2019 ukilinganisha na mwaka 2018.Dk Msonde alisema maandalizi kwa ajili ya mtihani hiyo imekamilika ikiwa in pamoja na kusambazwa kwa mtihani husika, vijitabu vya kujibia na nyaraka zote muhimu zinazohusu mtihani hiyo katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani.Aidha, alitoa mwito kwa kamati za mtihani za mikoa na halmashauri, manispaa na majiji kuhakikisha kuwa taratibu zote za uendeshaji mitihani ya taiga zinazingatiwa ipasavyo.Alizitaka kamati hizo kuhakikisha kuwa mazingira ya vituo vya mitihani yapo salama, utulivu na kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha kutokea kwa udanganyifu.“Kamati zote zinaelekezwa kuhakikisha usalama wa vituo teule unaimarishwa na kwamba vituo hivyo vitumike kwa kuzingatia mwongozo uliotolewa na baraza. Tunatoa mwito kwa wasimamizi wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu,” alifafanua.Kwa mujibu wa Dk Msonde, wasimamizi wanaelekezwa kufanya kazi yao kwa weledi na kwa kuzingatia kanuni za mitihani na miongozo waliyopewa.Hata hivyo, alisema wasimamizi wanapaswa kuhakikisha wanalinda haki za watahiniwa wenye mahitaji maalumu haki hizo ni pamoja na kuwapa mitihani yenye maandishi nukta nundu kwa watahiniwa wasioona na maandishi yaliyokuzwa kwa watahiniwa wenye uoni hafifu.
3
Mwandishi Wetu,Dar es Salaam ZAIDI ya wafanyabiashara 2000 katika mkoa wa kodi wa Ilala wamepatiwa elimu ya kodi inayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini.Mamlaka hiyo imekuwa na ikifanya kampeni ya elimu ya kodi mara kwa mara kwa kuwafata wafanyabiashara kwenye biashara zao (mlango kwa mlango). Akizungumzai zoezi hilo Afisa Msimamizi wa Kodi wa mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Zakeo Kowelo alisema kuwa katika siku sita za zoezi hilo, jumla ya wafanyabiashara 2,165 wamepatiwa elimu mbalimbali ya kodi. Alisema maeneo ambayo wamewafikia wafanyabiashara na kuwapatia elimu ni Tabata, Relini, Bima, Liwiti, Barakuda, Kimanga, Segerea, Kinyerezi, Kisiwani na Bonyokwa Mkoa wa Kodi wa Ilala. Alisema zoezi limeenda vizuri na kwamba wafanyabiashara wametoa ushirikiano wa kutosha kwa kutoa taarifa muhimu na kuonyesha nyaraka ambazo zilihitajika jambo ambalo limewawezesha kuwapa ushauri na elimu inayostahili. “Kwa hili tunawashukuru sana kwani tumeweza kuwaelimisha kama tulivyopanga”, alisema KoweloAlisema zoezi lilihusisha kupita duka kwa duka na kuangalia taarifa za wafanyabiashara za kodi ambapo baada ya kuangalia taarifa walifanya majadiliano na kumshauri mfanyabiashara jinsi ya kutunza kumbukumbu. Aliongeza kuwa kwa wale ambao hawajasajili biashara zao wameelekezwa taratibu za kusajili ili watambulike kuwa walipakodi na kwamba pamoja na kusajili biashara pia wafanyabiashara wameshauriwa jinsi ya kujisajili na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na wale wanaostahili kutumia mashine za kodi za kielektroniki wamepewa utaratibu wa kupata na kuzitumia mashine hizo. “TRA ni sehemu ya biashara za wananchi hivyo lengo letu ni kuwaelimisha wananchi ili wafanye biashara kwa usalama zaidi na kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi sahihi na kwa wakati’, alisema Kowelo. Naye Stewart Kimbaga mfanyabiashara wa duka la urembo maeneo ya Bonyokwa alisema kuwa kampeni hiyo ya elimu ya kodi ni nzuri na kwamba itasaidia kutokana na kuwa baadhi ya wafanyabiashara hawana uelewa wa jinsi ya kufanya biashara ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kulipa kodi. Alisema hiyo ni fursa muhimu na kwamba ukaguzi peke yake hautoshi bali unatakiwa uambatane na elimu ili kuwaongezea wananchi uelewa na kujenga uhusiano mzuri baina ya TRA na walipakodi. Zoezi la kutembelea walipakodi katika maeneo yao ya biashara ni mkakati ambao TRA inautekeleza ili kuwaelimisha walipakodi, kuwapa ushauri wa kitaalamu kuhusu taratibu za kulipa kodi, kusajili biashara ambazo hazijasajiliwa, kuwakumbusha kulipa kodi, kutatua changamoto zinazo wakabili na kupata maoni yao kuhusu huduma inayotolewa na TRA kwa ajili ya kuboresha utendaji wake.
5
Umejikita kuhakikisha Tanzania inajenga uchumi wa viwanda na kuongeza kiwango cha ajira na uzalishaji. Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Thomas Samkyi aliyasema hayo wakati akizungumza na wanahabari Dar es Salaam jana.Alisema, benki hiyo imeamua kusaidia utekelezaji huo ili kuwezesha upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini. Pia, alisema umenuia kuleta mapinduzi ya kilimo kutoka kwenye cha kujikimu kuwa cha kibiashara, hivyo kuchangia kukuza uchumi na kupunguza umasikini.“Ili kuhakikisha tunaunga mkono sera ya kujenga uchumi wa viwanda nchini, benki ya kilimo itatoa mikopo ya zaidi ya Sh bilioni 40 kwa wakulima. Itakuwa ni ya muda mfupi, wa kati na mrefu, kwa riba nafuu ya kati ya asilimia saba hadi 12 kwa mwaka,” alisema Semkyi.Alisema mikopo hiyo inalenga kuwanufaisha wakulima wadogo, wa kati na wakubwa kwa ajili ya kuziba pengo la upatikanaji wa fedha za kwenye mnyororo wa ongezeko la thamani katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na mazao ya misitu.Pia TADB itasaidia upatikanaji wa malighafi kwa viwanda vya ndani hivyo kusukuma ndoto ya serikali kufikia lengo lake la kujenga uchumi wa viwanda. Benki hiyo pia imelenga kuongoza katika utoaji mikopo kwa viwanda vidogo na vyakati vya usindikaji na uchakataji mazao ya kilimo na mifugo katika kuyaongezea thamani kwenye shughuli za kilimo.Pia, alisema benki hiyo tangu kuanzishwa imetoa elimu kwa wakulima na kuwawezesha kupata mikopo kupitia vikundi vya ushirika 89 vilivyopatiwa elimu mkoani Iringa, vyenye wakulima 21,526.Upande wa mikopo kwa wakulima ilishatoa mikopo kwa vikundi nane vya wakulima 857 na sasa inashughulikia maombi ya mikopo kwa awamu nyingine yenye thamani hiyo. Mkurugenzi wa Mikopo na Usimamizi wa Biashara wa Benki hiyo, Robert Pascal alisema, kwa miradi mikubwa ya kilimo inayoendeshwa kati ya serikali, taasisi za serikali na sekta binafsi, mikopo ya moja kwa moja itatolewa kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya kilimo hasa kuimarisha mifumo ya minyororo ya kuongeza thamani katika mazao.Pascal alieleza kuwa benki hiyo itatumia bidhaa mbalimbali zenye ubunifu katika kuwezesha vikundi vya wakulima wadogo, wafugaji wa ng’ombe, samaki na kuku. Aidha, alisema benki hiyo inatarajia kuwafikia Watanzania wengi zaidi hasa vijana wanaojishughulisha na kazi za kilimo kwa kuwapatia mikopo lakini kupitia vikundi.Alisema TADB inataraji kuvifikia vikundi zaidi ya 100,000 ambavyo katika kila kikundi kinaundwa na wanachama takribani 100, hivyo wanataraji kutoa mchango mkubwa zaidi katika sekta ya kilimo hasa kupitia kundi la vijana.
5
KINARA wa mabao Ligi Kuu Bara, Salim Aiyee wa Mwadui hajajumuishwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars chini ya kocha Emmanuel Amunike, suala ambalo amekiri limezidi kumuongezea hasira na changamoto ya kufanya vizuri zaidi ili wakati mwingine ajumuishwe katika kikosi hicho.Aiyee, ambaye ana mabao 15 dhidi ya wapinzani wake wa karibu; Meddie Kagere wa Simba na Heritier Makambo wa Yanga, ambao kila mmoja amefunga mara 12, tofauti ilivyotarajiwa na wengi mshambuliaji huyo hajajumuishwa katika kikosi hicho kinachojiandaa kucheza dhidi ya Uganda kuwania kushiriki michuano ya Afcon.“Hapo awali sikuwahi kuitwa Stars kwa hiyo kwangu si kitu cha kushangaa sana ingawa kwa kasi na juhudi nilizonazo msimu huu wengi walitarajia itakuwa hivyo, pamoja na hayo naona bado nina nafasi ya kuitwa katika siku za usoni.Stars ipo Kundi L katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 5 sawa na Lesotho iliyo nafasi ya tatu.Kinara ni Uganda yenye pointi 13 wakati Cape Verde ikiwa ya mwisho na pointi zake nne. Stars itahitaji ushindi katika mchezo huo huku ikiombea Lesotho ifungwe na Cape Verde.
4
London, England KOCHA wa timu ya taifa ya Italia, Antonio Conte, ana matumaini ya kuthibitishwa kuwa kocha wa muda mrefu wa timu ya Chelsea, kabla ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Hispania Machi 24, mwaka huu. Kocha huyo anaamini anaweza kutua kwenye klabu hiyo na kupata mkataba wa miaka mitatu na kuwazidi makocha wengine waliokuwa wakihitajika na klabu hiyo. Wawakilishi wake ambao walikuwa kwenye mazungumzo na uongozi wa Chelsea bado wanaendelea na mazungumzo hayo, ambapo msingi wake ni kupatikana kwa kocha atakayechukua nafasi ya kocha wa mpito wa sasa, Guus Hiddink, mwishoni mwa msimu. Mkataba wa kuifundisha timu ya taifa ya Italia unakwisha mwishoni mwa msimu huu baada ya michuano ya Ulaya hivyo kocha huyo huenda akapewa mkataba mpya kutoka Shirikisho la Soka la Italia (FA). Italia watakutana na Hispania na baada ya siku tano watakutana na Ujerumani, ambapo Conte angependa hadi wakati huo dili lake liwe tayari limekamilika kabla ya michezo ya kirafiki ya kimataifa kuanza. FA imekuwa katika mchakato wa kuandaa mkataba mpya wa kocha huyo ili kubaki na timu ya taifa hadi Kombe la Dunia mwaka 2018, lakini Conte (46) anaonekana kuwa na hamu ya kutaka kutua Chelsea. Awali Chelsea ilikuwa na matarajio ya kuinasa saini ya kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeon, Jorge Sampaoli na Massimiliano Allegri, lakini imeonekana kuwa Conte ndiye chaguo lao la kwanza. Kupatikana kwa kocha wa timu hiyo inaweza kuwa nafasi ya Juan Cuadrado, ambaye anatumikia usajili wake wa mkopo kwenye klabu ya Juventus. Cuadrado anatarajia kupata usajili wa moja kwa moja na miamba hiyo ya Italia, lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 bado anayo nafasi ya kumshawishi kocha mpya wa Chelsea. Hata hivyo, kwenye tukio jingine Mkuu wa Ufundi wa Chelsea, Michael  Emenalo, alionekana kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uliokuwa ukichezwa na Juventus dhidi ya Bayern Munich, ambapo walikutana na Conte huku kukiwa na taarifa ya usajili wa Paul Pogba na Arturo Vidal majira ya kiangazi.
4
MTOTO wa miaka minne, Ittai James mkazi wa Dar es Salam, aliyekuwa akiugua saratani ya tumbo ameonyesha dalili za kupona baada ya madaktari bingwa wa Hospitali ya Narayana ya India, kumfanyia upandikizaji wa uroto.Hospitali ya Muhimbili Mloganzil, Dar es Salaam itaanza kupandikiza uroto kwa wagonjwa wa saratani na wenye selimundu mwezi ujao.Ittai alipandikizwa uruto Septemba, 2019 nchini India.Mkurugenzi wa Hospitali ya Narayana Health wa India Dk Sunil Bhat amesema Itanni alikuwa kwenye hatua ya mwisho ya ugonjwa huo lakini hospitali hiyo imefanikiwa kumpa tiba iliyoonesha mafanikio katika kipindi cha wiki tatu.Baba mzazi wa mtoto huyo James Moshi ambaye ni mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) amesema alimpeleka mwanawe Bengaluru, India mwishoni mwa mwaka 2018 kwa matibabu baada ya kusumbuliwa na homa kali, mwili kumuuma na maumivu ya tumbo.“Hakuna matibabu yaliyomsaidia licha ya kwenda kwenye hospitali tofauti tofauti hapa nchini, Oktoba 2018 hakuweza hata kutembea,”amesema Moshi.Amesema hospitali hiyo ya Narayana kwa mara ya kwanza ilianza kumtibu maambukizi ya bakteria yaliyosambaa hadi katika mifupa na ndipo jopo la madaktari wakaamua kumfanyia vipimo vikubwa vya uchunguzi na akabainika na saratani.“Tulipata taarifa kuwa hospitali ya Narayana ina uwezo wa kutibu saratani hii. Nina furaha kumuona mwanangu kwa sasa anacheza na anafurahi,” amesema mama mzazi wa mtoto huyo Scholastica Musokwa.Akizungumzia upasuaji wa mtoto huyo kabla ya kumpandikiza uruto Dk Bhat amesema walimuondoa uvimbe uliokuwa na dalili za saratani Julai 2019 na Septemba mwaka jana na wakampandikiza seli za damu kutoka kwenye uroto wa mwilini mwake.Naibu Mkurugenzi wa Muhimbili, Julieth Magandi amesema kuanza kutolewa kwa huduma hiyo nchini itasaidia kutibu wanachi wengi zaidi hasa wenye saratani.Kuhusu gharama amesema wanaokwenda kutibiwa nje ya nchi ni Sh milioni 200 kwa anayepandikizwa uroto kutoka kwa ndugu yake, wakati kwa anayepandikizwa wa kwake mwenyewe hugharimu hadi Sh milioni 150.“Kwa mwaka, watu 130 hadi 150 wanahitaji huduma hii na theluthi mbili ya wagonjwa hufariki dunia kila mwaka kwa kukosa huduma hiyo ambayo gharama yake ni kubwa”amesema.Magandi amesema utoaji wa huduma hiyo nchini utapunguza idadi ya vifo na pia itaipunguzia serikali gharama ya kupeleka wagonjwa kutibiwa nje ya nchi.Pia gharama za tiba zitapungua kwa asilimia 50 kutoka kwenye gharama za kutibia nje ya nchi hivyo Muhimbili imejipanga kuhudumia wagonjwa wote wa ndani na nje ya nchi watakaokuja kutibiwa kuanzia mwezi ujao yaani February.Dk Magandi amesema kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, huduma hiyo itakuwa ikipatikana Muhimbili Mloganzila kwa kushirikiana na Muhimbili Upanga ambako vipimo vyote vitakua vikipatikana hapo wakati matibabu ni Mloganzila pekee na hivyo hospitali hiyo imejipanga kuwahudumia pia wagonjwa kutoka nchi za jirani.Kwa mujibu wa Dk Magandi huduma hiyo ya uroto ni ya kupandikiza chembechembe mama za kuzalisha damu, ambazo hupatikana kwenye uroto au kutoka kwenye chembechembe mama kwenye kitovu cha mtoto mchanga au kondo la nyuma la mama.Amesema njia inayotumika zaidi ni ya kupandikiza chembechembe mama za damu kutokea kwenye uroto itawasaidi wagonjwa wote wanaopatwa na changamoto ya damu hasa zitokanazo na saratani.
3
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua channel mpya ya utalii ya shirika la utangazaji TBC, ijulikanayo kama Tanzania Safari Channel. Chaneli hiyo mpya itatoa maudhui mbalimbali yanayohusiana na vivutio vua utalii nchini.Akizungumza kwenye uzinduzi huo uliofanyika kwenye ofisi za TBC, Mikocheni jijini Dar es Salaam, Waziri Majaliwa ameeleza kuwa channel hiyo itakuwa chachu kubwa ya kutangaza vivutio vya utalii nchini na kuongeza idadi ya watalii wanaokuja kuvitembelea.“Tanzania kwa mwaka inapokea watalii takriban milioni 1.3, idadi ambayo ni ndogo ukilingalisha na nchi nyingine duniani kama Misri ambayo hupokea hadi watalii milioni 10 kwa mwaka,” alisema.Waziri Majaliwa aliongeza kuwa kwa mwaka jana, 2017, utalii umetuingizia Taifa dola za Marekani bil 2.3/- sawa na tril 5.04/- za Kitanzania hivyo watalii wakiongezeka pato la taifa litakuwa zaidi.Alisema pia kuwa sekta ya utalii ikiboreshwa itatengeneza ajira zaidi ya milioni 1.5 kwa Watanzania, huku ikizingatiwa kuwa serikali ina malengo ya kuongeza watalii hadi kufikia milioni 2 ifikapo mwaka 2020.
3
LONDON, ENGLAND BAADA ya mchezaji wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thierry Henry, ambaye alikuwa kocha wa vijana wa timu hiyo kutangaza kujiuzulu, nafasi hiyo imechukuliwa na aliyekuwa nyota wa klabu hiyo, Tony Adams. Henry ameachana na jukumu la kuwa kocha wa vijana baada ya kupishana kauli na kocha Arsene Wenger, baada ya kocha huyo kumtaka achague moja kati ya ukocha au uchambuzi katika kituo cha Sky Sports. Henry mbali ya kuwa kocha, lakini aliajiriwa na kituo hicho cha utangazaji huku akiwa kama mchambuzi wa michezo, lakini Wenger alishangazwa kumuona nyota huyo akifanya kazi ya uchambuzi na muda mwingi anautumia kuwafundisha vijana ila siku za mwisho wa wiki anawakosoa wachezaji. Kauli hiyo ya Wenger ilionekana kumgusa nyota huyo na kuamua kuachana na jukumu la ukocha na kubaki kwenye uchambuzi ambapo katika kazi hiyo analipwa pauni milioni 4 kwa mwaka. Kutokana na Henry kujiuzulu, nafasi hiyo inachukuliwa na aliyekuwa mchezaji wa klabu hiyo, Adams ambaye aliitumikia Arsenal kwa miaka 19 akiwa kama mchezaji, huku akifunga mabao 32 katika michezo 504 aliyocheza. Hata hivyo, Henrry ameitakia kila la heri Arsenal ya vijana ikiwa na kocha mpya pamoja na ile ambayo ipo chini ya Wenger. “Napenda nimshukuru Andries Jonker kwa kunipa nafasi ya kuifundisha Arsenal ya vijana kwa kipindi chote nilichokaa, hata hivyo napenda kumshukuru Arsene Wenger kwa maamuzi yake, hivyo nawatakia kila la heri katika mafanikio ya klabu,” alisema Henry. Mtandao wa Sky Sports, umedai kwamba Henry atabaki kukumbukwa katika ulimwengu wa soka kutokana na kile ambacho amekifanya katika kipindi chake.
4
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala amesema Rais Dk. John Magufuli amemaliza kazi 2020, kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM. Akizungumza katika mahojiano maalumu mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na televisheni ya Star TV, Kilakala alisema anaamini kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambao ndiyo mkataba baina ya chama na wananchi, hadi kufikia mwaka 2020 Rais magufuli atakuw hana deni tena na wananchi. “Hadi sasa kuna mambo mengi yamefanyika katika sekta zote, ikiwemokatika sekta za elimu, afya, miundombinu na sekta ya maji, kwa hiyo niseme hadi ikifika 2020, Rais Magufuli atakuwa hana deni tena na wananchi,” alisema. Alisema kwenye sekta ya afya, katika miaka minne ya utawala wa Rais Magufuli amejenga hospitali mpya 69 za wilaya zilizogharibu Sh bilioni 1.5 zinazotokana na mapato ya ndani. Alisema hiyo ni hatua kubwa kwa kuwa tangu uhuru hadi kufikia mwaka 2015, katika kipindi chote hivho zilijengwa hospitali 77 tu za wilaya, hivyo ujenzi wa hospitali 69 katika kipindi cha miaka minne ni jambo la kipekee. Alisema tayari ndani ya muda wa uongozi wa Rais Magufuli amejenga vituo vipya vya afya zaidi ya 352, vitu ambavyo mwanzo havikuwepo. Alisema tayari shule mpya zimejengwa katika ameneo yote ya nchi na shule kongwe zimekarabatiwa na kuwa za kisasa zaidi, huku wananchi wakifaidika na sera ya elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi sekondari. Kilakala alisema kupitia Ilani ya Uchaguzi mwaka 2015, CCM iliaminiwa na wananchi wengi kupitia ilani yake ya uchaguzi ambayo ni ni mkataba wa chama na wananchi kwa hiyo inaendelea kusimamia ilani hiyo kuhakikisha inatekelezwa ikiwa imefikia katika hatua nzuri. Alisema kwa sasa, yale yaliyobebwa na Ilani ya chama iliyobebwa na Rais Magufuli na kunadiwa kwa wananchi ambao waliielewa na kukipa chama hicho ridhaa ya kuongoza kwa sasa imetekelezwa kwa kiasi kikubwa. Hali ya demokrasia Kuhusu kuminywa kwa demokrasia nchini, Kilakala alisema demokrasia haijaminywa na Serikali ya Rais Magufuli ambayo ni wazi kwamba inaongoza katika suala la utawala bora. “Tunapozungumzia vyama vya siasa kufanya shughuli zake, tangu Rais Magufuli alipoingia madarakani hajazuia mikutano ya hadhara na kila mbunge wa chama anatakiwa kufanya shughuli za kisiasa katika maeneo yake,” alisema. Alisema ajenda ya CCM kwa sasa ni maendeleo na mafanikio, ni kuwafuta machozi wananchi na kuwashughulikia wananchi kuhakiksha wanapatana maendeleo. Alisisitiza kwamba sera walizozinadi kupitia ilani ya chama hicho zipo kwenye mkataba wao na wananchi, ambao ndio waliowapa ridha kwa kishindo. “Sera ya CCM kwa wananchi ni kutaua kero zao na kuhakikisha wanapata kwa uhakika huduma zote muhimu za msingi. “lakini zaidi kuna haki ya demokrasia katika nchi yetu na CCM inaamini kuwa maendeleo hayana chama, ndiyo maana pamoja na kwamba Rais hajapata kura nyingi katika Mkoa wa Dar es Salaam lakini anatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika mkoa huu,” alisema. Alisema pia kuwa ni wajibu wa vijana kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuwania nafasi kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ili kuonyesha uwezo wao katika uongozi. Akizungumza katika mahojiano maalumu mwishoni mwa wiki, Kilakala alisema ni wazi kwamba mahitaji ya vijana kwa sasa ni mengi na hakuna wa kuwatetea kama hawajaamua kujitetea wenyewe. Alisema aliona ni vyema kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais  Magufuli, kwa kuwa imeonyesha imani kubwa kwa vijana na kuwataka vijana waliopewa nafasi za uongozi kuhakikisha kuwa hawamuangushi. “Na sasa, katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ni wajibu wa vijana kujitokeza na kuchukua fomu na kugombea. Mahitaji ya vijana ni mengi katika taifa hili. “Sasa hivi tuko wengi, mahitaji yetu ni mengi, tujitafakari na kuchukua hatua. Hakuna mtu yeyote anayeweza kututetea kama sisi wenyewe hatujaamua kujitetea,” alisema. Maendeleo bila itikadi Alisema kwa kauli ya Rais, alisema amewasamehe waliochagua upinzani na kwamba CCM na serikali yake kazi yake ni kupeleka maendeleo katika maeneo yote ya nchi bila kujali chama. Kilakala alieleza kuwa kungekuwa na uwezekano wa kususia maendeleo kwa sababu Jiji la Dar Salaam linaongozwa na upinzani, lakini kwa kuthamini kwamba wananchi wote wana haki sawa kupata maendeleo na kuthaminiwa utu wao, Serikali haiwezi kuwa ya kibaguzi. Alisema CCM inaamini binadamu wote ni sawa na kila mtu ana haki ya kuthaminiwa na kutambuliwa utu wake, hivyo isifike mahala mtu yeyote akanyanyaswa kwa sababu alikuwa upinzani, kwa kuwa jukumu lao ni kuongoza nchi na wananchi, bila kuangalia chama, dini, kabila au rangi. Alieleza kuwa katika teuzi zake, CCM inaangalia uwezo, weledi na uchapakazi wa mtu, kwa hiyo anaamini hili wimbi la wapinzani kuhamia CCM ni ishara kuwa wameujua na kuufanhamu ukweli kwa sababu hata viongozi wakuu waliowania urais 2015 wamehamia CCM. “Kwa hiyo hii inamaanisha kuwa yale waliyoyatarajia wangeyafanya kama wangepewa ridhaa tayari yanafanywa na Rais Magufuli. Kuna wabunge pia ambao waliona kuwa yale waliyoyatarajia na kuyasema majimboni kwao tayari yanatekelezwa na Rais Magufuli. “Kwa hiyo haina sababu ya kuendelea kupinga, mimi nipongeze maamuzi yao ya kujua ukweli na kuunga mkono juhudi,” alisema. Alisisitiza kuwa wabunge na wanachama kutoka upinzani waliojiunga na CCM ni kwa sababu wameufahamu ukweli na wametumia vizuri demokrasia. Wabunge kununuliwa Alisema anashangazwa na propaganda kuwa wabunge wanaotoka upinzania na kurudi CCM wamenunuliwa na kuhoji mbona aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu alipotoka CCM kwenda upinzani hakuna aliyesema amenunuliwa. Alisema katika mkakati maalumu wa Tanzania ya kijani ulioasisiwa na UVCCM unamaanisha Tanzania ya CCM, ikiwa na lengo la maalumu kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa “Mkakati huu umefanikiwa kwa asilimia kubwa na matokeo yake yataonekana wazi Novemba 24, ambapo tutashinda kwa zaidi ya asilimia 90 kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa,” alisema. Alisema vijana sasa hivi wanathaminiwa na wamepewa nafasi za juu za uongozi kitaifa. Amani nchini Alisema vijana wengi waliopo sasa wameukuta Uhuru na wameukuta Muungano, mambo yanayowafanya Watanzania waishi kwa amani, umoja na mshikamano, kwa sababu ya uasisi uliofanywa na Baba wa Taifa, Julius Nyerere na Abeid Amani Karume. “Leo hii tunajivunia kwa sababu Mungu aliwapa maono hayo. Hatubaguani kwa rangi dini wala kabila, wote tunapendana na tunaishi wamoja. “Wote tunaishi pamoja, kwa mfano hapa Dar watu tunaishi kwenye nyumba ya vyumba sita kila chumba kina mtu wa dini, imani na kabila tofauti na wanaishi salama, tukipoteza amani hii hatuna mahala pa kukimbilia,” alisema. Alisema ni wajibu wa vijana kuhakikisha kwamba wanailinda amani hii na kutumia nguvu zote kuhakikisha wanailinda amani na hawatumiwi kwa namna yoyote kuharibu amani hii. Alisema ni suala la kushukuriu kwa kupata viongozi wenye nia ya dhati kuitoa Tanzania hapa ilipo kuipeleka mahala pengine, hivyo wanahitaji kuungwa mkono kwa dhati. Alisema wapo wanawaombea mabaya viongozi wao, lakini wanatakiwa kutambua kuwa Mungu huwa hapokei dua mbaya na kwamba wanapowaombea wenzao mabaya watarajie ndiyo wanapata mafanikio.
3
Mchezaji huyo kwa sasa yupo katika wakati mgumu hasa kutokana na utata uliogubikwa kuhusu mkataba wake na klabu yake hiyo, ambapo kwa upande wake anasema kuwa mkataba wake umemalizika huku klabu hiyo ikisema kuwa bado anao mwaka mmoja wa kuendelea kuwatumikia.Akizungumza na gazeti hili, Messi alisema kuwa kwa jina linavyosikika katika vyombo vya habari ni tofauti kabisa na kiwango cha maisha anayoishi, kwani anaishi kwa dhiki sana.Alisema kwa mchango wake katika medani ya soka hapa nchini alikuwa akitakiwa kuishi maisha ya kati au hata ya juu kabisa kutokana na namna ambavyo amesaidia kuanzia timu yake hadi timu ya Taifa.Alisema kuwa kwa sasa anaendelea kuishi kwa kaka yake Hamis Ramadhan waliozaliwa baba mmoja na mama tofauti huku chumba hicho ni mali ya kaka yake huyo ambapo wanatumia chumba kimoja.Wanaishi eneo la Keko Machungwa na hali ya chumba hicho ni cha kawaida huku wakiwa wanaishi mazingira ya kawaida kabisa, kwa upande wake alisema kuwa aliahidiwa kuwa angepewa kodi ya nyumba kila mwezi lakini hajapewa hadi sasa.Alisema kuwa hata baada ya kuandika barua mara kwa mara za kukumbushia suala hili, hakuna lolote alilofanyiwa kazi hadi sasa na ndio sababu za kutaka kuondoka klabuni hapo.Alisema kuwa hali kama hiyo inatokana na sababu mbalimbali huku sababu kubwa, ikiwa ni kushindwa kupewa fedha stahili kama sehemu ya mshahara pamoja na mapato mengine.Alisema kuwa akiwa kama mchezaji wa mpira kwenye klabu kubwa ambayo imeitumikia kwa muda mrefu alikuwa akistahili kuishi katika mazingira ambayo yanamwezesha kufanya mengi kama mwanamichezo.Aliongeza kuwa katika maisha hayo ya kukaa chumba kimoja na kaka yake yanamwathiri pia kisaikolojia hasa akiangalia ni kwa namna gani wachezaji wenzake ambavyo wanaishi."Mimi naweza kusema kuwa ni vema tu hata hivyo mkataba umeisha nikaondoka na kupata mwelekeo wa soka mahala pengine ili angalau niweze kusonga mbele zaidi kimaisha labda mapato yatakuwa angalau," alisema mchezaji huyo.Aliongeza: "Nimeanza kucheza soka muda mrefu hadi kuja kusajiliwa na klabu ya Simba na nilikuwa najua kuwa mambo yanakuja kuwa safi ila dah, naona kama kazi bado ni kubwa mno," alisema mchezaji huyo.Mchezaji huyo ambaye ameonesha nia ya kuihama klabu hiyo kama njia mojawapo ya kujitafutia maisha na ameonesha nia ya kuhamia klabu ya Azam FC, alisema kuwa ameshangazwa na kitendo cha kuwapo kwa mikataba miwili tofauti kuhusiana na utumikiaji wake kwenye klabu ya Simba.Alisema kuwa kwa mkataba alionao yeye unamuonesha kuwa anatakiwa kuitumikia klabu hiyo kwa miaka miwili huku ule uliopelekwa katika ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), unaonesha kuwa ana mkataba wa miaka mitatu.Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba, Zakaria Hanspoppe alikiri klabu hiyo kudaiwa na mchezaji huyo, lakini alisema linazungumzika na kila kitu kitakuwa sawa.Alisema kuwa Messi ni mchezaji mwenye mchango mkubwa sana kwa timu hiyo na hakuna sababu ya kumwacha na kuna kila sababu ya kumsikiliza na kufuatilia malalamiko yake.Hali kama hiyo inampatia wakati mgumu mchezaji huyo kuhamia klabu nyingine kwa sasa suala hilo lipo kwenye Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji.Kuhusu kutaka kujiunga na Azam FC, juzi msemaji wa klabu hiyo Jaffar Idd alisema kuwa kwa sasa hawana haja na mchezaji huyo hadi pale atakapomalizana na klabu yake ya sasa.
4
Kwan hamna wenye ukimwi wanene ?????? Msikalili Ni moja ya comment aliyandika costanciapatrc  moja ya mtumiaji wa mtandao kwenye post ya mwanadada Wema Sepetu  kufuatia alot of comments za watumiaji wa mtandao kudai kuwa mwanadada huyo sio mzima kwa kile wanachoona kama kakonda sana. Katika siku hivi karibuni kwenye post za mrembo Wema Sepetu kumeibuka wingi wa comments kutoka kwa shabiki zake juu ya hali aliyokuwa nayo tofauti na alivyoozeleka. Mtumiaji mwingine aitwae Rozamkenya alimshauri pia aende medical checkup ya nguvu na kama hospital za Bongo hazifanyi kazi aende Kenya kwa checkup. Mmmh! Watu wanamaneno aisee! Wengine walienda mbali na kukumbushia kuwa msanii huyo wa maigizo nchini alishawahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006 na umbo alilonalo hii leo alikua nalo enzi zile. Mtumiaji wa mtandaoa bizzo_for_real yeye ndo alikuja na theory huku akiungwa mkono na watu wengi mtandaoni, bizzo_for_real aliandika; Wembamba huo naona umezidi kuwatesa watu wengi mtandaoni na hata wengine kufikia hatua ya kumtaka bora angeendelea kuwa nyumbu kuliko alivyo sasa. Hizi hapa nyingine baadhi ya comment kwenye moja ya post yake My Sexy Self… . . Dressed by my dada @jacquescollection . . Hair by @luluzhair Styled by @americannailstz A post shared by Wema App (@wemasepetu) on Feb 23, 2020 at 2:08pm PST Sikiliza hapa mwenyewe akifunguka juu ya kukonda kwake;
1
WIZARA ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo (DP), imeanza mchakato wa kuanzisha Bima ya Mazao (BM) hapa nchini.Akiwalisha bajeti ya Wizara ya Kilimo bungeni jana, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga (pichani) alisema kilimo ni moja ya maeneo yenye changamoto kubwa ya kupatikana hasara katika uwekezaji.Hasunga alisema kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo za ukame, mafuriko, magonjwa na wadudu waharifubu wanaoweza kuharibu mazao nchini, yanatakiwa kuwekewa bima. Alisema changamoto za mazao zimekuwa sikisababisha taasisi mbalimbali za fedha kutotoa kipaumbele cha kutosha katika kutoa mikopo kwenye sekta ya kilimo.“Katika kukabiliana na changamoto hizo, nchi nyingi duniani zimeanza na kutekeleza mfumo wa bima ya mazao,” alisema na kuongeza kuwa mfumo huo wa kutoa bima ya mazao, humuwezesha mkulima kulipwa fidia pale anapopata hasara na pia kumuwezesha kupata mkopo kutoka vyombo vya fedha kwa urahisi. Hasunga alisema wizara kwa kuanza imeshafanya vikao na wadau ili kufanya maandalizi ya awali ya kuanzisha utaratibu wa Bima ya Mazao (BM) kwa kuanza na baadhi ya mazao na maeneo machache.Alisema maandalizi hayo, yanaendelea kufanyika ili katika mwaka 2019/20 kuwe angalau na aina mbili za mifumo ya Bima ya Mazao inayoweza kutumika nchini. Hata hivyo ili utaratibu huu uwezekane, zinahitajika takwimu sahihi za hali ya hewa pamoja na uzingatiaji wa kanuni bora za kilimo na kuongeza kuwa ushirikiano wa karibu na mamlaka ya hali ya hewa pamoja na maofisa ugani kutimiza wajibu wao kikamilifu unahitajika.Alisema wizara hiyo pia ilianza utaratibu wa kuwatambua, kusajili na kuwapatia vitambulisho wakulima nchini. Utambuzi huo ulianza kupitia mazao ya biashara yanayosimamiwa na Bodi ya Mazao ambapo usajili huo utakamilika Juni mwaka huu. Aliongeza kuwa katika mwaka 2019/20, wizara itaimarisha kanzidata ya wakulima na kuendelea na usajili wa wakulima wa mazao mchanganyiko kwa kushirikina kwa karibu na vyama vya ushirika na taasisi nyingine za wakulima kama vile Tanganyika Farmers Association (TFA).Alisema kwa kutamua umuhimu wa masoko nchini, wizara imeamua kuimarisha utafutaji wa masoko ya mazao ya kilimo ndani na nje ya nchi. Vile vile alisema wataendelea kufanya kazi kwa karibu na taasisi nyingine zinazohusika masoko ikiwemo Tantrade na Soko la Bidhaa (TMX). Katika hatua nyingine, mazao 10 yamewekewa mkakati wa kuimarishwa na kuongeza uzalishaji wake kufikia tani takribani milioni 25 katika mwaka 2019/20 kutoka tani milioni 19 zilizofikiwa katika mwaka 2017/18.Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga alisema wizara hiyo inaratibu mkakati wa kuimarisha utafiti, upatikanaji na utumaji wa pembejeo na zana za kilimo, udhibiti visumbufu vya mazao, huduma za ugani, uongezaji wa thamani na upatikanaji wa masoko. Ili kuongeza uzalishaji huo wa takribani tani milioni 5.7, Waziri Hasunga alisema katika mwaka 2019/20, wizara imejipanga kuongeza uzalishaji wa mahindi kutoka tani 6,300,000 zinazozalishwa sasa hadi tani 8,000,000.Pia imejipanga kuongeza uzalishaji wa mpunga kutoka tani milioni 3.385 katika mwaka 2017/18 hadi tani milioni 4.36 katika mwaka 2019/20. “Wizara imepanga kuongeza uzalishaji wa ngano hadi kufikia tani 85,000 kutoka 56,651 zilizozalishwa mwaka 2017/18,” alisema na kuongeza kuw akwa upande wa muhogo mbichi imejipanga kuongeza hadi tani milioni 10 kutoka tani milioni nane za mwaka 2017/18.Kwa mujibu wa waziri Hasunga, wizara pia imejipanga kuendeleza alizeti ili kutosheleza mafuta ya kula kwa kuongeza uzalishaji kutoka tani 768,188 katika mwaka 2017/18 hadi 820,905. Hasunga alisema wizara kupitia TARI, ASA, Jeshi la Kujenga Taifa, Magereza, Sekretariati za Mikoa na sekta binafsi zitazalisha miche ya michikichi milioni tano kwa ajili ya kuongeza uzalisaji wa zao hilo. Aidha, wizara itashirikiana na Sido, Carmatec, NDC na FAO/UNIDO kuwapatia wakulima zana bora za uzalishaji na uongezaji thamani zao hilo la michikichi.Aidha, bodi kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango itahakiki na kulipa vikundi vya wazalisha miche ya mikorosho 2017/18 kutoka mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani, Tanga, Dodoma na Singida. Alisema wizara imejipanga kupitia Bodi ya Sukari kuongeza kuzalisha sukari tani 403,786 kwa kuongeza eneo la uzalishaji wa kilimo cha miwa kutoka hekta 52,000 hadi hekta 97,000.“Wizara kupitia Bodi ya Kahawa itaongeza uzalishaji kutoka tani 65,000 hadi tani 80,000 na itashirikiana na wadau kuongeza matumizi ya mitambo ya awali ya kuchapata kahawa kutoka asilimia 35 hadi 50,” alisema. Kuhusu mkonge, wizara kupitia bodi ya zao hilo, imepanga kuongeza uzalishaji kutoka tani 38,506 hadi tani 113,426 kwa kuongeza eneo la uzalishaji kutoka hekta 42,426.11 hadi 114,91.08 ili kuongeza mauzo nje ya nchi kutoka asilimia 24.5 hadi 35.5. “Wizara kupitia bodi ya pamba imepanga kuongeza uzalishaji wa zao hilo kutoka tani 220,000 hadi tani 700,000.Bodi pia imepanga kuongeza ubora wa pamba kutoka asilimia 43 hadi 75,” alisema. Alisema wizara kupitia Bodi ya Tumbaku imepanga kuongeza uzalishaji kutoka tani 55,000 hadi 60,000 pamoja na kukamilisha usajili wa wakulima wa zao hilo kwa kutumia mfumo wa kieletroniki na kuimarisha vituo 1,972. Wizara kupitia bodi ya chai imejipanga kuongeza uzalishaji chai kavu kutoka tani 34,000 hadi 40,000 ambazo ni sawa na 182,000 za majani mabichi ya chai.
3
BAADA ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kumtaka Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad, kufi ka mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kujibu tuhuma za kulidhalilisha Bunge kuwa ni dhaifu, wanasheria na wasomi wamefunguka kuhusu suala hilo.Ndugai alivieleza vyombo vya habari jijini Dodoma juzi kuwa CAG pamoja na Mbunge wa Kawe jijini Dar e s Salaam, Halima Mdee (Chadema) ambaye aliunga mkono kauli ya CAG kuwa Bunge ni dhaifu, wanapaswa kufika mbele ya Kamati hiyo Januari 21 na 22, mwaka huu. Gazeti hili jana liliripoti kuwa Desemba 30 mwaka jana, Profesa Assad wakati akifanya mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, alisema kuwa Bunge la Tanzania ni dhaifu, kwa kuwa limeshindwa kuzifanyia kazi ripoti za ufisadi, zinazotolewa na ofisi yake.Kauli hiyo ya CAG, ilimuibua Spika Ndugai aliyedai kuwa CAG ndiye anayepotosha, kwa kuwa haiwezekani aiseme nchi yake vibaya anapokuwa nje ya nchi, hivyo kuagiza CAG na Mdee kufika kuhojiwa na wasipotekeleza wito huo, hatua nyingine zitachukuliwa dhidi yao. Kutokana na hali hiyo, Wakili wa Kujitegemea, Albert Msando, alilieleza gazeti hili jana kuwa wakati CAG anatekeleza wajibu wake kisheria, hawezi kuhojiwa kwa jambo lolote na mtu yeyote, kwa kuwa sheria inamlinda.Hata hivyo, alisema kwa upande mwingine wa shilingi, Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, inaeleza kuwa mtu yeyote, bila kujali nafasi yake, hapaswi kulidharau au kulikashifu Bunge na akifanya kosa hilo, Spika anaweza kumuita ili kuhojiwa na kamati hiyo. Ili kujua nguvu aliyonayo CAG ya kulindwa na sharia, lakini pia na nguvu iliyonayo Bunge ya kumhoji mtu yeyote anayelidharau, gazeti hili lililazimika kutafuta tafsiri ya kisheria na utawala bora juu ya muktadha huo.Msando alisema katika suala hilo la Spika na CAG, kilichotakiwa kuangaliwa kwanza ni tafsiri ya neno ‘dhaifu’ kama ni kweli neno hilo linalidhalilisha Bunge au la. Alisema kama tafsiri ambayo ilipaswa kuangaliwa, ingethibitisha ni kweli neno hilo linalidhalilisha Bunge, basi ndipo Bunge lingekuwa na sababu ya kumwita CAG kwa mahojiano.“Sasa swali ni kwamba nani mwenye mamlaka kisheria ya kutafsiri neno ‘dhaifu’ kama linalidhalilisha Bunge au la? Hapa kingepaswa kiundwe chombo kingine huru cha kutoa tafsiri na si Bunge lenyewe ambaye ni mlalamikaji kufanya kazi hiyo. Bunge haliwezi kuwa mlalamikaji na mwamuzi lenyewe, na katika kipengele hiki, sheria iko kimya”alieleza Msando. Kwa mujibu wa Msando, kwa kuwa CAG alitoa kauli hiyo wakati ambao hakuna Bunge linaloendelea, hajalidhalilisha Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 24 cha Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.“Spika alipaswa kulipeleka jambo hili kwenye mamlaka iliyomteua CAG yaani Rais na kulalamika kuwa amelidhalilisha Bunge katika vyombo vya habari, ndipo mamlaka iliyomteua CAG ingepima na kutoa uamuzi,” alieleza Msando. Wakili huyo alisema kuwa Spika alipaswa kumfikishia wito huo CAG kimaandishi, akiweka hoja zote ambazo CAG anatakiwa kuzitolea ufafanuzi katika utetezi wa kauli yake ; na si kueleza jambo hilo kwenye vyombo vya habari. Alisema hata kama CAG atakwenda kuhojiwa, bado Bunge haliwezi kisheria kumshauri Rais atengue uteuzi wake, ila linachoweza kufanya ni kutoa karipio tu.Msando alisema kwa kuwa Bunge na CAG wanafanya kazi kwa karibu na kwa kushirikiana, kama itaonekana jambo hilo linaleta ukakasi katika kutimiza majukumu yao, ndipo sasa Rais mwenyewe anaweza kuamua ama aendelee naye au amtoe au yeye CAG mwenyewe, aamue kwa hiari yake kujiuzulu kutokana na hali ya kutoaminiana kati yake na Bunge. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye ni Mtaalamu wa Sayansi ya Siasa, Dk Benson Bana, alisema kuwa uamuzi wa Bunge kumwita CAG na kutaka kumhoji ni sahihi, kwa kuwa kauli yake ya kwamba Bunge ni dhaifu, aliitoa akiwa nje ya ofisi yake.Alisema CAG anapaswa kuwa makini na kauli zake, kwa kuwa yeye ni sehemu ya serikali, hivyo ana wajibu wa kuhakikisha mwenendo, kauli na tabia yake vinaendana na dhana ya utawala bora, ikiwemo kuheshimu mihimili mingine ya dola. Mihimili ya dola ni Mahakama, Bunge na Utawala (Serikali). “Kwa kweli kauli ya kusema Bunge ni dhaifu inachefua. Kauli kama hii inapaswa kutolewa mahali sahihi na si hadharani kama hivyo, kwa hiyo ni sahihi kwa Spika Ndugai kumwita ili ahojiwe ili kujua kauli yake ina mwelekeo gani, na CAG si kiongozi wa kwanza kuitwa na Bunge kwa sababu hata Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alishawahi kuitwa na kuhojiwa na Bunge,”alieleza Dk Bana.Majukumu ya Kamati ya Haki na Maadili ya BungeKanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Januari 2016 Nyongeza ya Nane Kifungu cha 4 (1) (a) na (b), kinaeleza kuwa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itatekeleza majukumu yake kwa: Kuchunguza na kutoa mapendekezo kuhusu masuala yote ya haki, kinga na madaraka ya Bunge, yatakayopelekwa na Spika ; na kwamba itashughulikia mambo yanayohusu maadili ya Wabunge yatayaopelekwa na Spika.Kamati hiyo itakapokamilisha kushughulikia jambo husika, Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika kwa maandishi kwamba Kamati imemaliza kujadili jambo husika na Spika baada ya kupokea taarifa hiyo, ataagiza iwekwe kwenye Orodha ya Shughuli za Bunge kwa ajili ya kuwasilishwa na kujadiliwa bungeni.Kinga ya CAG kikatibaHali ikiwa hivyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Ibara ya 143 (6) inasema kwamba, katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2), (3) na (4) ya ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali.Lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo, hayataizuia Mahakama kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au sivyo.Katiba inavyoweza kumwondoa CAGKwa mujibu wa Ibara ya 144 (1), CAG atalazimika kuacha kazi yake atakapotimiza umri wa miaka sitini au umri mwingine wowote, utakaotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge.Na Ibara ya 144 (2) inaeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu anaweza kuondolewa katika madaraka ya kazi yake, kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake, ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote, au kwa sababu ya tabia mbaya, au kwa kuvunja masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; na hataweza kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya 4 ya ibara hii.Nafasi ya Rais katika kumwondoa CAGRais ana mamlaka kikatiba ya kumwondoa CAG kwa mujibu wa Ibara ya 144 (3)(a) (b). Ibara hiyo inasema kuwa iwapo Rais ataona kwamba suala la kumwondoa kazini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kwa mujibu wa masharti ya ibara hii linahitaji kuchunguzwa, basi atateua Tume Maalum ambayo itakuwa na Mwenyekiti na Wajumbe wengine wasiopungua wawili. Kwa mujibu wa ibara hiyo, Mwenyekiti na walau nusu ya wajumbe wa Tume hiyo wanapaswa kuwa watu ambao ni Majaji au watu waliopata kuwa Majaji wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufani katika nchi yoyote iliyomo kwenye Jumuiya ya Madola.Ibara hiyo inafafanua kuwa Tume hiyo itachunguza shauri lote na kisha kutoa taarifa kwa Rais kuhusu maelezo ya shauri lote na itamshauri Rais kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, aondolewe kazini kwa mujibu wa masharti ya ibara hiyo kwa sababu ya kushindwa kufanya kazi kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya.
3
JOSE Mourinho ameibuka na kuzitabiria mabaya timu nne za Ligi Kuu ya England zilizofuzu kwa hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya akidai kuwa zote zitatolewa, huku fainali zikicheza Barcelona na Juventus.Manchester United imepangwa kucheza na Barcelona katika robo fainali na mshindi atacheza ama na Liverpool au Porto. Kwa upande mwingine wa ratiba hiyo ya robo fainali, Tottenham itakwaana na Manchester City katika mchezo utakaozikutanisha timu zote za uingereza na mshindi wa mtanange huo atacheza ama na Juventus au Ajax katika nusu fainali nyingine.“Juventus na Barcelona ni timu mbili kubwa katika kinyang’anyiro hicho na ndio watakaofika hatua ya fainali, “alisema Mourinho, ambaye alitupiwa virago na Man United Desemba mwaka jana.“Wote wanazungumza kuhusu [Cristiano] Ronaldo na [Lionel] Messi lakini mimi napenda kuzungumzia kuhusu Juventus na Barcelona. Wakati wote nitaendelea kuwa kocha wa soka na soka litaendelea kuwa mchezo wa timu na sio mchezo wa mchezaji mmoja mmoja. “Juventus na Barcelona zinauzoefu, vipaji na hasa kwa kila mchezaji. Na kuna hawa wachezaji maalum, timu inaishia kuwa bora kutokana na wachezaji hao.”
4
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema ameridhishwa na kasi na viwango vya ujenzi wa mfumo wa Reli ya Kisasa (SGR) inayojengwa na Kampuni ya Yapi Merkezi ya Uturuki.Makonda ameyasema hayo alipotembelea mradi wa ujenzi wa reli hiyo ya kisasa kipande cha kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro chenye urefu wa kilometa 300, akiambatana na kundi la watu zaidi ya 600 kutoka fani tofauati wakiwemo wasanii.“Nimeridhishwa na viwango na maendeleo ya ujenzi kwa sehemu ulivyofikia pamoja na ushiriki wa Watanzania wengi katika mradi huu, tunataka muendelee kujenga kwa kasi hii,” amesema Makonda.Amesema serikali inataka kuona malengo ya Rais John Magufuli ya kutaka kuona SGR inakamilika na kuanza kutumika nchini yanatimia.“Nimedokezwa hapa asilimia asilimia 96 ya watu walioajiriwa katika mradi huu ni Watanzania, hii ni fursa nzuri, wote mliambatana nami naamini mtakuwa mabalozi wazuri kuzungumzia mradi huu na miradi mingine mbali mbali inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano,” alisema.Awali, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa alisema awamu ya kwanza ya mradi huo wa reli kutoka Dar es Salaam hadi Makutupora unagharimu Sh trilioni 7.1.Kadogosa alisema mradi wa ujenzi wa reli hiyo yenye urefu wa kilometa 1,219 kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza umegawanyika katika vipande vitano, kipande cha kwanza ni kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro chenye urefu kilometa 300 na unagharimu Sh trilioni 2.7.“Kipande kingine ni kutoka Morogoro hadi Makutupora chenye urefu wa kilometa 422 ambacho kinagharimu Sh trilioni 4.4, Makutupora hadi Tabora kilometa 376.5, Tabora hadi Isaka kilometa 162.5 na Isaka hadi Mwanza kilometa 311.25,” alisema Kadogosa.“Utandikaji wa reli umeshaanza hadi sasa zaidi kilomita 15 zimetandikwa. Na zoezi la utandikaji bado linaendelea.”Mhandisi wa mradi kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro, Machibya Masanja alisema mradi huo utakuwa na vivuko 17 vya juu na vivuko 15 vya chini sambamba na madaraja.Alisema katika eneo la Soga Mkoa Pwani itakuwa kiungio cha reli hiyo ya umeme ambako reli ya kisasa itapita juu na ile ya kawaida itapita chini.Alisema katika kipande cha Dar es Salaam – Morogoro, mbali ya kazi ya kutandika reli, kazi nyingine zinazoendelea ni ujenzi wa madaraja, makaravati, kuzalisha mataruma, ujenzi wa miundombinu ya ishara ya mawasiliano na nguzo za umeme.Kwa upande wa mataruma uzalishaji umeanza katika kiwanda kilichopo eneo la Soga mkoani Pwani na kiwanda hicho kinatarajia kuzalisha mataruma 1,200,400 kwa kipande cha Dar es Salaam – Makutupora.Kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro yatazalishwa mataruma 500,100 na kipande cha Morogoro – Makutupora mataruma 703,300.“Mataruma tunazalisha hapa nchini kwa kutumia malighafi kutoka katika viwanda vyetu. Taruma moja lina uzito wa kilo 380 hivyo tunahitaji saruji nyingi na tunapeleka mchango katika viwanda vyetu,” alisema Machibya.Katika eneo la Mzenga na Mlandizi, ujenzi wa makutano ya barabara na reli kuwezesha watu na magari kuvuka kwenda upande mwingine tayari umekamilika ambapo barabara itapita chini na treni juu.Alisema stesheni ziko sita na stesheni kubwa zitakuwa Dar es Salaam na Morogoro wakati stesheni ndogo zitakuwa Pugu, Soga, Ruvu na Ngerengere.“Stesheni zetu zimesanifiwa kwa kufuata mazingira halisi ya nchi yetu, Dar es Salaam itakuwa na umbo la Tanzanite ya Morogoro imechanganywa kwa nyumba za asili na Milima ya Uluguru,” amesema.Hata hivyo, Machibya ame  sema katika Bonde la Mto Ruvu kuna changamoto ya udongo wa mfinyanzi, hivyo wamekata kina cha mita 2.5 kwa ajili ya kuweka mawe na kuboresha udongo ili kujenga tuta imara la reli. Katika eneo hilo pia kutajengwa madaraja sita.Maeneo mengine korofi yako kwenye Milima ya Kilosa ambayo inatakiwa kupasuliwa kuwezesha treni kupita chini.Mkuu wa Kitengo cha Habari TRC, Jamila Mbarouk amesema jumla ya wafanyakazi 6,440 wameajiriwa katika mradi huo ambao Watanzania ni 6,182 sawa na asilimia 96 na wageni ni 258 sawa na asilimia 4.Amesema reli hiyo itakapokamilika itaongeza kasi ya ukuaji wa uchumi hasa katika sekta ya usafirishaji kwani treni moja itakuwa na uwezo kukimbia spidi 160, akitolea mfano Dar es Salaam mpaka Morogoro kufika ni dakika 90 na pia kusafirisha tani 10,000 sawa na malori 500 yenye uzito wa tani 20 kila moja.
3
WABUNGE wameonesha kiu ya kuona Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), ukiongezewa fedha kutoka asilimia 30 ya sasa hadi kufi kia asilimia 50, ili kuboresha mtandao wa barabara vijijini.Maoni hayo yalitolewa na wabunge kadhaa wakati wa kuchangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na Utumishi na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2019/20. Akichangia Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje (CCM) aliishauri serikali kutatua changamoto ya fedha kwa Wakala hao na kuangalia uwezekano wa kuuongezea fedha kutoka asilimia 30 za sasa hadi kufikia asilimia 40 hasa kutokana na umuhimu wa barabara za vijiji katika kusafirisha mazao na abiria.“Naishauri Tamisemi ili iangalie kuongeza fedha kwa ajili ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini. Pia ziangalie barabara za Mpwapwa ni mbaya sana,” alisema. Lubeleje pia aliishauri serikali kuangalia upya mfumo wa fedha za kodi kukusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kudai kuwa fedha hizo zimekuwa zikichelewa kurudishwa kwenye halmashauri jambo linalochelewesha utekelezaji wa miradi ya halmashauri.“Halmashauri zina miradi, na fedha zinakuwa TRA mwaka mzima halafu baadaye ndio halmashauri ziweze kupata hizo fedha, nashauri Tamisemi, hili mliangalie upya angalau miezi sita halmashauri ziweze kupata mgawo wa fedha zao,” alieleza. Naye, Mbunge wa Segerea, Bonnah Kamoli alisema Tarura ndio Wakala wenye mtandao mkubwa wa barabara upatao kilomita 130,000 ikiwa ni tofauti na Tanroads yenye kilomita 30,000 hivyo kuna haja kwa Tarura kuongezewa fedha.“ Naomba nishauri serikali waweze kubadili sheria ili watu wa Tarura waongezewe fedha, Dar es Salaam tuna matatizo makubwa ya barabara, ukiangalia jimbo la Segerea tuna barabara moja ya lami iko kata ya Kimanga, hivi sasa inajengwa kwa muda wa miaka minne kutokana na tatizo la bejati,” alisisitiza.Alisema endapo Tarra wataendelea kutengewa asilimia 30 ya bajeti ni wazi kuwa wakala huyo atashindwa kutekeleza baadhi ya miradi. Kimoli pia alitaka kuwepo na mipango ya mapema kwa kuandaa miundombinu katika shule za umma ili kuendana na kasi ya ongezeko la wanafunzi. Pia pamoja na kuipongeza serikali kutoa Sh milioni 500 kwa kituo cha afya na aliomba serikali kujenga kituo cha afya kingine hasa kutokana na kuwa jimbo hilo lina wakazi zaidi ya milioni moja.Naye, Mbunge wa Muleba Kasikazini, Charles Mwijage (CCM) alisema tiba ya kuhakikisha barabara za vijijini zinajengwa ni kwa kuanzisha mfuko wa barabara ambao ndio utatumika kutengeneza mtandao wa barabara za vijijini. Mbunge wa Mufindi Kaskazini, Mahamoud Mgimwa (CCM) alisema wabunge wanaotoka vijijini wana matatizo makubwa ya barabara kuliko wale wa mjin.Alieleza kuwa fedha zinazopelekwa Tarura ni kidogo hivyo kupendekeza mgawo uwe asilimia 50-50 na kuwa isipofanywa hivyo watakwamisha namna ya kusafirisha malighafi na mazao ambayo kwa asilimia kubwa hutokea vijijini.Naye, Mbunge wa Viti Maalumu, Zainabu Mdolwa (CUF), mbali na kutaka Tarura kuongezewa fedha, aliishauri serikali kupitia Wizara ya Tamisemi kuondoa tozo ya kuhifadhi maiti katika hospitali kwa sababu imekuwa kero kwa wananchi, “Ikumbukwe kwamba marehemu huyo pia alikuwa analipa kodi serikalini kupitia kununua bidhaa mbalimbali akiwa hai, watoe tozo ya kuhifadhi maiti tunaona maeneo mengi waliondokewa na ndugu zao huchelewa kuchukua miili kutokana na kiwango kikubwa cha kulipa,” alisema.
3
Na ADAM MKWEPU-DAR ES SALAAM        |      KUKOSEKANA chombo makini cha kusimamia mchezo wa masumbwi nchini kumesababisha ushindwe kupiga hatua, badala yake umezidi kurudi nyuma na kupoteza mwelekeo. Ukosefu wa chombo makini umesababisha kuwapo kwa migogoro ya mara kwa mara ambayo imeathiri ukuaji wa mchezo huu, ambao huko nyuma ulikuwa ukipendwa na Watanzania wengi, lakini kubwa ulililetea sifa Taifa letu la Tanzania. Kupitia mchezo huu, Tanzania iliweza kujitangaza vema nje ya mipaka yake kutokana na wabondia wake kutamba katika mapigano ya kimataifa. Mabondia walikuwa wakijitoa kwaajili ya taifa lao na taasisi mbalimbali, hasa majeshi zilikuwa mstari wa mbele kuwaunga mkono. Majina kama Rashid Matumla, marehemu, Stanley Mabesi ‘Ninja’ na Michael Yombayomba, ni baadhi ya mabondia walioipeperusha vema Bendera ya Tanzania katika medani ya kimataifa, kutokana na kushinda mataji kadhaa. Walichokifanya mabondia hao kinaendelea kuenziwa na kukumbukwa na wadau wa soka hapa nchini. Kizazi cha sasa cha akina Francis Cheka kimejitahidi kupambana, lakini kimeshindwa kufanya yale yaliyofanywa na Matumla na wenzake nje ya mipaka ya Tanzania. Hata hivyo, baada ya taasisi, hasa za kiserikali kuacha kusapoti mchezo huu, umeathirika kwa kiasi kikubwa. Hakuna tena vipaji vipya vya maana ambavyo vimekuwa vikizalishwa, kwakuwa mabondia chipukizi wamekuwa hawapati mahitaji ya msingi yanayoweza kuwafanya wawe bora zaidi. Ukata ni tatizo sugu kwa sasa katika mchezo wa masumbwi na kuhatarisha maendeleo yake. Ukweli ni kwamba, mchezo wa ngumi umeshuka thamani machoni mwa Watanzania na wadau wa mchezo huo na kuondoa heshima yake kwa waliokuwa wakiupenda. Mapromota hawapendani, mabondia wanafanyiana figisu, viongozi wa mashirikisho ndiyo usiseme, kila mmoja ana kundi au upande wake, bila kujali kama unafanya vizuri au vibaya. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, ameonyesha nia ya dhati katika kurejesha heshima ya mchezo huu pamoja na kutatua migogoro iliyodumu kwa kipindi kirefu. Tangu mwishoni mwa mwaka 2017, Waziri Mwakyembe amekuwa na vikao mfululizo na wadau wa mchezo huu, akilenga kutafuta mwarobaini wa matatizo yanayoufanya usipige hatua. Tayari Dk. Mwakyembe ameunda mfumo mpya wenye lengo la kulinda maslahi ya mabondia na wadau wengine wa mchezo huu. Mwakyembe ameunda Kamati ya Mpito ambayo itashirikiana na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), kuhakikisha kila kitu kinakwenda vizuri katika mchezo huu. BMT itahakikisha hakuna bondia anayesafiri nje ya Tanzania kupigana bila kupata kibali maalumu kutoka kwake. Waziri Mwakyembe pia yupo katika hatua ya mwisho ya kukabidhi katiba, ambayo itakuwa msingi utakaosimamia mchezo wa ngumi za kulipwa hapa nchini. Akizungumza hivi karibuni wakati akipokea mrejesho uundwaji wa katiba mpya itakayosimamia mchezo wa masumbwi, Mwakyembe anasema: “Naapa kwa Mungu nitausafisha mchezo wa ngumi na hakuna atakayeweza kupambana na Serikali. “Ukiwa na chombo mahususi cha kusimamia mchezo huu, hakuna migogoro itakayojitokeza, haya yote yanayotokea yanatokana na kila chama cha ngumi kuwa na uhuru wa kufanya wanavyojisikia”. Mwakyembe anasema kamati ya mpito aliyoiunda inalengo la kusaidia kupata katiba mpya ya mchezo wa ngumi za kulipwa nchini. Anasema kilichobaki kwa sasa ni kuitisha mkutano wa wadau wa masumbwi ambao unatarajiwa kufanyika Juni, mwaka huu, ili kuikabidhi katiba hiyo. “Haya yote yanafanyika kwa kuwa mchezo wa ngumi umegubikwa na vitendo vya jinai na vurugu. “Katika vitendo, hivyo kuna watu wameumia na wengine wamefaidika. “Tunataka mikataba iwekwe juu ya meza, kwani kwa kukosa uelewa baadhi ya mabondia hukatwa fedha nyingi kwa kuwa hawana mwongozo wala wanaowapigania,” anasema Waziri Mwakyembe. Naye promota wa mchezo huo, Shomari Kimbau, anaipongeza Serikali kwa kuonyesha nia ya dhati ya kusaidia mchezo wa masumbwi nchini. “Lazima yawepo mazingira mazuri ya kusimamia mchezo huu, ili upendwe na watu wengine pamoja na kurudisha imani kwa wadau na wawekezaji waweze kuwekeza fedha zao. “Hiki kinachofanywa na Serikali ni kitu kizuri na kinafaa kuungwa mkono na wadau wa mchezo huu,” anasema Kimbau. Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), Yassin Abdallah, anasema kinachofanywa na Serikali kitakuwa na faida kubwa, kama kweli kitatekelezwa kikamilifu. “Serikali ndiyo kila kitu, kama imeamua kuusimamia mchezo huu huenda kukawa na mabadiliko makubwa, ikiwamo kurudisha heshima iliyopotea kwa muda mrefu,” anasema Abdallah. Wakala na bondia wa zamani, Chaurembo Palasa, anasema kabla Dk. Mwakyembe hajaonyesha matamanio yake katika kuusaidia mchezo huo, uligubikwa na vurugu nyingi kutokana na kukosa utaratibu mzuri. “Kwenye mchezo wowote duniani utaratibu ni jambo jema, lakini hata kama kukiwa na chama kimoja lazima watu watakaoongoza wawe na uzoefu. “Mchezo huu ulivurugika kutokana na kuwapo na vyama vingi vya ngumi ambavyo vilikuwa vikisababisha kuwapo kwa makundi ambayo yalikuwa yakitetea maslahi binafsi,” anasema Palasa.
4
Kutokana na leseni hiyo, sasa benki hizo mbili zitakuwa zikijiendesha zenyewe huku wakikabiliwa na changamoto ya mtaji ambapo kwa utafiti wao, wanahitaji Sh bilioni 500 kwa miaka mitano, lakini Serikali imewapatia Sh bilioni 110 hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali kupata fedha hizo.Wakurugenzi watendaji wa benki hizo mbili, Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo, Peter Noni na Mkurugenzi wa Benki ya Biashara, Frank Mugeta, walitangaza rasmi jana katika Maonesho ya 39 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) kuwa na benki hizo zinazojitegemea tangu Juni 24, mwaka huu.Akizungumza jana, Noni alisema Serikali imetenga Sh bilioni 30 katika bajeti zake kila mwaka kwa lengo la kuongeza mtaji kwa ajili ya kutoa huduma za maendeleo, ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika miundombinu ikiwepo reli na barabara.Alisema wanaishukuru Serikali ya awamu ya nne kwa kufanikisha mchakato huo, ulioanza baada ya kuingia madarakani na wamekamilisha wakiondoka kwa lengo la kuondoa umasikini na kusaidia pato la wananchi kukua toka asilimia saba hadi 15.Alisema benki hiyo inakuwa katika mikopo kwani mwaka jana walitoa Sh bilioni 100 na mwaka huu wanatarajia kutoa mikopo ya Sh bilioni 200.Noni alisema benki hiyo imefanikiwa kuanzisha Benki ya Kilimo ambayo inatarajiwa kuanza hivi karibuni kutoa huduma, ikiwemo mikopo kwa wakulima pamoja na kuwezesha Shirika la Reli Tanzania (TRL) Sh bilioni 12 kwa ajili ya kufufua treni na dola za Marekani milioni 18 kutengeneza vichwa vya treni vilivyochakaa na tayari kazi imeanza.Alisema pia wametoa mkopo wa dola za Marekani milioni 26 kwa ajili ya kuzalisha gesi mkoani Mtwara, kwa Kampuni ya Wentinorth na kutengeneza bomba la gesi kwa ajili ya kusafirisha gesi asilia na kupunguza gharama za umeme.Alisema pia katika kutoa msaada kwa jamii wanashirikiana na Kampuni ya Phils kutoka nchini Dubai, kwa ajili ya uwekezaji kwa kushirikiana na Manispaa za Jiji na wanawekeza Sh bilioni 10 kutengeneza miundombinu.
5
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Raymond Mbilinyi alitoa mwito huo kwa wajumbe wa Baraza la Biashara la Mkoa wa Ruvuma hivi karibuni mjini hapa.Alisema wakati umefika kwa halmashauri kuainisha maeneo yote muhimu yenye fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji.“Mkutano huu na wadau wote wa baraza ambao unawajumuisha wajumbe kutoka halmashauri zote za mkoa huu ni vyema mnaporudi kwenye maeneo yenu ya kazi mkafanya mchakato wa kuainisha fursa zote,” alisisitiza Mbilinyi.Alisema Baraza linaamini endapo halmashauri zitaibua fursa za biashara mapato ya Serikali yataongezeka.Pia ajira kwa vijana zitaimarika hivyo kipato kwa Watanzania kukua. Katika kikao na waandishi wa habari, Mbilinyi alisema “Huu mkoa una kila sababu za kujivunia katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwani una ardhi ya kutosha yenye rutuba na mvua ya kutosha pia.”Alisema mbali na kilimo, Mkoa wa Ruvuma una madini ya urani, makaa ya mawe na maeneo mazuri ya kuvutia utalii wa ndani na nje ya nchi.“ Mkoa huu ni tajiri sana, kila kitu kipo jambo kubwa ni kwa watendaji wa halmashauri kuweka mazingira mazuri ya kufanya biashara na kuvutia zaidi uwekezaji katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kubadilisha maisha ya watu,” alisema.Alisema kuwepo kwa Baraza la Mkoa ambalo linajumuisha wajumbe kutoka sekta za umma na binafsi, itakuwa chachu kubwa ya kuongeza kasi ya kimaendeleo katika wilaya zote mkoani hapa.Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Ernest Kahindi, alisema wilaya yake inategemea uvuvi kuingiza kipato katika halmashauri hiyo na kusema kuwa lengo lao kwa sasa ni kuwawezesha vijana kwa kuwapatia zana za kisasa za kuvulia samaki.Mwenyekiti wa Chama cha wenye Viwanda Biashara na Kilimo ( TCCIA) Wilaya ya Tunduru Mohamed Kiondo alisema Baraza hilo limewapa mwamko katika kuhimiza kilimo katika wilaya zao.Alisema mkoa unategemea kilimo hususani tumbaku, korosho na mahindi ambayo kwa mujibu wake, mazao hayo yanaingiza fedha nyingi. “Baraza hili ni fursa pekee ya kujitangaza,” alisema Kiondo.
5
HALMASHARUI ya Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara imekabidhiwa kinyago cha masikitiko kutokana na kufanya vibaya kwa kuwa wa mwisho kimkoa katika matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2018. Kinyago hicho kimepokelewa na Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, Dua Nkurua kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC).Akikabidhi kinyago hicho hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa alisema kwa kitendo hicho ni ushahidi tosha kwa wakazi wa Nanyumbu kuwa bado hawafanyi vizuri kwenye elimu.Mbunge wa Jimbo hilo wakati akipokea kinyago hicho alisema kuwa, amekiri kupokea kinyago kwa masikitiko ambapo wanachukulia kama changamoto ambayo wataifanyia kazi kwa kuhakikisha mwaka kesho hawapokei tena kinyago.Ametoa sababu inayopelekea kutofanya vizuri katika matokeo hayo ikiwemo wazazi kushindwa kuwasimamia vema watoto wao, upungufu wa watumishi katika halmashauri hiyo hivyo kupelekea kushindwa kulisimamia vema suala hilo pamoja na kukosekana kwa lishe shuleni.Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu, Moses Machali alisema kuwa, wilaya hiyo imekuwa ikijitahidi kupanda kielimu kwa kufanya mambo mbalimbali ikiwemo kuboresha miundombinu ya elimu na ufundishaji kwa kuwaondoa walimu wakuu wasiofundisha kwa kutumia utaratibu unaotakiwa.“Tumepiga hatua kwenye sekta ya elimu matokeo ya elimu ya msingi ya mwaka jana ya darasa la saba wilaya yetu ilikuwa inaufaulu kwa asilimia 51 na tumetoka asilimia 51 tukaenda asilima 72 mpaka 73 mwaka 2018.“Kwahiyo hatujarudi nyuma tunazidi kwenda mbele ukiangalia kwamba historia ya wilaya ya Nanyumbu kidogo ni eneo ambalo lilikuwa liko nyuma kwahiyo kuna hatua tunasogea kwahiyo ongezeko la ufaulu kwa asilimia 20 siyo haba lakini ukija kupima kuna mafanikio na maendeleo katika matokeo ya ufaulu katika sekta ya elimu”,Katibu tawala wilayani humo Palango Salum alisema, jambo hilo ni la heri kwa wilaya hiyo kwani ni moja ya njia ya kuongeza bidii na kujifunza. Alisema kinyago hicho wilayani humo kitawasaidia kujipanga ili kupiga hatua zaidi ambapo moja ya mkakati waliojiwekea ikiwemo usimamizi wa walimu katika suala la mahudhurio lakini pia kushirikisha jamii katika kuhakikisha kwa pamoja wanasimamia jambo hilo.Katika matokeo hayo wilaya ya Nanyumbu imeshika nafasi ya mwisho kati ya halmashauri tisa za mkoa wa Mtwara na kitaifa na fasi ya 136 kati ya halmashauri 185.Sanjari na hilo mkuu huyo amekabidhi zawadi kwa shule ambazo zimefanya vizuri katika matokeo hayo ya darasa la saba ambapo shule ya msingi Macdonald iliyopo wilaya ya Masasi ambayo imekuwa ya kwanza kimkoa.
3
Na Leonard Mang’oha-Dar es Salaam JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia Meneja wa Maabara wa Tume ya Madini, Donald Njonjo (30), kwa tuhuma za kuiba dhahabu  kilo 6.244 yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 507 iliyokuwa imehifadhiwa ofisi za Wakala wa Madini Masaki, Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari Dar  es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alisema Juni 29, mwaka huu walipata taarifa kutoka kwa Ofisa Madini Mkoa wa Dar es Salaam, Ally Sadick baada ya kugundua kuibwa madini hayo. Kamanda Mambosasa alisema baada ya kupata taarifa hizo, jeshi hilo lilianza uchunguzi mara moja na kubaini kuwa madini hayo yaliibwa na Njonjo na kuwa alianza kuyaiba tangu Desemba mwaka jana. Alisema baada ya mtuhumiwa kuhojiwa, alikiri kuiba madini hayo kidogo kidogo kutoka katika ofisi za Tume ya Madini. “Mtuhumiwa alieleza kuwa madini hayo aliyauza katika duka la kuuzia vito vya dhahabu na kisha kuhifadhi madini bandia yenye uzito wa kilo 6.001 nyuma ya jengo la Tume ya Madini ili kuyapeleka katika chumba walichoiba madini hayo halisi kuyabadilisha. “Madini hayo halisi ya dhahabu yalikamatwa mwaka 2017 huko maeneo ya bandarini Zanzibar yakiwa yanasafirishwa kinyume cha sheria kisha kutaifishwa na Serikali na kuhifadhiwa katika ofisi za Tume ya Madini. “Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linakamilisha utaratibu wa kupeleka jalada kwa mwendesha mashtaka wa Serikali ili mtuhumiwa afikishwe mahakamani,” alisema Kamanda Mambosasa. Wakati huohuo, jeshi hilo linawashikilia watu saba kwa tuhuma za wizi wa bajaji maeneo ya Ukonga. Kamanda Mambosasa amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Said Salum (27), Amo Kefas (30), Said Ahmad (38), Mohamed Musa (31), Mboke Samwel (26), Abdallah Kipaneli (25) na Mfaume Mussa (25). Alisema Julai 9 mwaka huu saa 8:00 usiku huko maeneo ya Kibeberu na Magole  Ukonga, watuhumiwa hao wanadaiwa walivunja maduka matatu na kuiba fedha pamoja na bidhaa mbalimbali zikiwamo bajaji mbili zenye namba za usajili MC 312 CFB na MC 540 CED zote aina ya TVS zikiwa na rangi ya bluu. “Baada ya wizi huo, taarifa zilipokewa katika Kituo cha Polisi Stakishari na upelelezi ulianza mara moja ambapo Julai 9, 2019 saa tano asubuhi watuhumiwa walikamatwa huko maeneo ya Hondogo Gogoni Kiluvya, Wilaya ya Ubungo. “Aidha watuhumiwa hawa wamekuwa wakifanya matukio ya uhalifu kwa kutumia gari aina ya Toyota Harrier nyeusi yenye namba T 666 DJG ambayo inashikiliwa na Jeshi la Polisi ili kubaini mmiliki wake,” alisema Kamanda Mambosasa. Alisema watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani hivi karibuni.
3
Petro alisema ujumbe wa mbio hizo ambazo mwaka huu zinatimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake ni kupiga vita ujangili wa wanyama.Alisema mbio hizo zitaanzia katika lango kuu la kuingilia na kutokea hifadhi ya Bonde la Ngorongoro na kumalizikia mjini Karatu katika Uwanja wa Mazingira Bora.Mbali na mbio za nusu marathon, pia kutakuwepo na mbio za tano pamoja na zile za 2.5, ambazo zitakuwa za watoto wadogo.Alisema kumekuwa na mauaji ya kinyama kwa wanyama kama tembo na faru, kwa ajili ya pembe zao huku twiga na pundamilia wakiuawa kwa ajili ya nyama zao.Petro alisema kuwa katika mbio za kilometa 21 wanariadha wa Tanzania watashiriki kwa Sh 5,000 wakati wageni watalipa dola za Marekani 50.Kwa upande wa mbio za kilometa 2.5 kwa watoto wale wa Tanzania watashiriki bure wakati wageni watatozwa dola tano za Marekani.Wakati wa shiriki wa mbio za kilometa tano, ambazo zitashirikisha wafanyakazi wa mashirika mbalimbali, washiriki watano hadi 10 watatoa dola za Marekani 1,500 huku mshiriki Mtanzania atatoa Sh 10,000 wakati mtanzania atalipa Sh 10,000.
4
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameagiza waliokuwa wafanyakazi wa Chama cha Ushirika katika eneo la Lambo Estate Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, kutoondolewa katika eneo hilo na kila mmoja kupatiwa ekari mbili kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kimaisha.Uamuzi huo wa Lukuvi wa kutoa ekari mbili kwa wananchi hao 78 unafanya jumla ya ekari 156 kati ya ekari 1600 kutolewa kwa wananchi. Uamuzi huo, unatokana na mgogoro wa muda mrefu baina ya waliokuwa wafanyakazi wa ushirika na uongozi .Mgogoro huo umeibuka baada ya wafanyakazi hao kutakiwa kuondoka katika makazi yaliyopo kwenye eneo la shamba kutokana na utumishi wao kukoma. Waziri Lukuvi alitoa maamuzi hayo leo katika wilaya Hai kiwa ni mwanzo wa ziara yake ya kutembelea wilaya za Hai, Moshi na Same kushughulikia migogoro ya ardhi katika wilaya hizo mkoa wa Kilimanjaro.Lukuvi alishangazwa na ushirika wa watu wachache kutaifisha ardhi na kuamuru watu waliokuwepo muda mrefu katika eneo la Lambo estate kuondoka na kusema kuwa safari hii serikali itawanyoosha wale wote wanaofanya ujanja wa kuwaonea wanyonge.“Sijawahi kuona ushirika wa namna hii ambapo wenye rasilimali hawanufaiki na ardhi iliyopo katika kijiji chao halafu ardhi hiyo inakodishwa kwa wanachama wa ushirika wanaotoka vijiji vingine,” alisema Waziri Lukuvi.Awali, Katibu wa jumuiya ya wana ushirika, Edward Chedi alimueleza Waziri Lukuvi kuwa mgogoro wa eneo hilo ulianza mara baada ya shamba hilo kutaifishwa na ajira za walikuwa wafanyakazi wa ushirika kukoma mwaka 2001.Baada ya hali hiyo, kulikuwepo na mfululizo wa kesi uliofikia ngazi ya Mahakama Kuu na kuagizwa waliokuwa wafanyakazi kulipwa mafao na kukabidhiwa vyeti vya kutambuliwa pamoja na ekari hamsini za kujikimu kwa kipindi watakachokaa hapo kabla ya kuondolewa.
3
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, ameagiza mradi wa ujenzi wa nyumba mbili za walimu katika chuo cha Ufundi Stadi (Veta), mkoani Njombe, unaotekelezwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) uchunguzwe.Amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka, kuchunguza mradi huo, baada ya kubaini kuwa pamoja na kupatiwa fedha nyingi na serikali mpaka sasa haujakamilika.Mradi huo wa nyumba mbili za ghorofa moja umegharimu kiasi cha Sh milioni 600 na tayari TBA wameshalipwa asilimia 90 ya fedha hizo lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea.Akizungumza baada ya kukagua miradi yote waziri Kamwelwe amemtaka Ole Sendeka kuuchunguza mradi huo wa miaka miwili ambao ulianza mwezi Oktoba, mwaka jana na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, mwaka huu lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea."Watu wa TBA wananisikitisha sana hasa ukiangalia wao wanafanya kazi kwa niaba ya serikali, tunazidiwa uwezo na wakandarasi binafsi hii ni aibu kabisa mkuu wa mkoa naomba usimamie ujenzi huu uhakikishe unakamilika," amesema.Kwa upande wake, Ole Sendeka alitoa siku saba kwa TBA, viongozi wa chuo, Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) na viongozi wengine wa mkoa wanaosimamia masuala ya ujenzi kufika ofisini kwake ili kuangalia namna ya kunusuru mradi huo uliogharimu fedha nyingi.Awali, akizungumza kwa niaba ya waziri Kamwelwe, Sendeka alisema huu ni wizi wa mchana ambao hauwezi kuvumiliwa hata kidogo kwa kuwa milioni 600 zinauwezo wa kujenga miradi mikubwa huku akitolea mfano zahanati ya Ipelele ambayo imekarabatiwa kwa kujengwa wodi, mochwari na vitu vingine vingi kwa gharama ya Sh milioni 400.
3
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali itaendelea kuiwezesha Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA), kuwa na vifaa na mitambo ya kisasa ya hali ya hewa ili kurahisisha huduma bora za utabiri kutolewa kwa wakati. Profesa Mbarawa amesema hayo mjini Dodoma leo Ijumaa Machi 23 na kusisitiza kuwa kwa sasa TMA imeongeza imani kwa wananchi kwani imekuwa ikitoa utabiri wa kuaminika kwa  sababu ya kuwa  vifaa vingi na vya kisasa vya utoaji taarifa. “Serikali itaendelea kuwezesha TMA na kuhakikisha inatoa utabiri sahihi na wa uhakika kwani kuwepo kwa utabiri sahihi kuwawezesha vyombo husika kuchukua hatua mapema kabla ya madhara makubwa kutokea,” amesema. Aidha, amewataka wananchi kutunza mazingira kwa kuacha kulima kwenye vyanzo vya maji na kuepuka kuchafua maeneo ya bahari ili kuepusha athari zinazoepukika zikiwemo uharibifu wa miundombinu ya  uchukuzi. “Nawaomba wananchi wote watunze mazingira kwani kumekuwa na uharibifu mkubwa wa miundombinu kutokana na shughuli zinazofanywa na binadamu katika maeneo mbalimbali yasiyotakiwa kulimwa au kujengwa, amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa. Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi amesema serikali inajitahidi kuwekeza kwenye miundombinu ya hali ya hewa kwa kutoa fedha kununua vifaa mbalimbali ambavyo vimewezesha mamlaka hiyo kutoa utabiri sahihi kwa zaidi ya asilimia 70. “Kwa sasa utabiri wa usafiri wa anga ni wa uhakika kwa asilimia 90 na hutolewa kila baada ya nusu saa na marubani hupata taarifa hizo kwa wakati kabla ya kuanza safari zao, amesema Dk. Kijazi.    
3
JESHI la Polisi nchini limewahakikishia raia wa kigeni wakiwemo watalii, kuwa nchi ipo salama dhidi ya vitendo vya kigaidi; na linaendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya nchi.Kauli hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime. Alisema hayo wakati akizungumzia hali ya usalama nchini, kwa kipindi hiki ambacho kumeibuka sintofahamu kati ya taifa la Marekani dhidi ya nchi za Iran na Iraki.Pia, kuwepo kwa taharuki kuhusu usalama wa raia wa Marekani na washirika wake duniani kote, hasa baada ya kutokea shambulio la kigaidi mjini Lamu, Kenya na kusababisha askari watatu na magaidi wanne kuuwawa.Mtafaruku huo umesababishwa na hatua ya Jeshi la Marekani, kumuua aliyekuwa Kiongozi wa Jeshi la Ulinzi wa Iran Nje ya nchi, Jenerali Qasem Soleiman wakati akiwa nchini Iraki katika ziara ya kikazi.Kutokana na hatua hiyo, vikundi mbalimbali vya kigaidi wakati wa maziko ya Jenerali Soleiman juzi, vilisisitizia msimamo wa kulipiza kisasi kwa Marekani.Tayari kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab cha Somalia, chenyewe kimeshambulia karibu na Kambi ya Kijeshi ya Simba iliyopo Lamu Kenya, kambi inayotumiwa na nchi za Kenya na Marekani.Pia jana nchini Iraki kambi mbili za Marekani, zililipuliwa kwa makombora 13 kutoka Iran na inadaiwa watu 80 wamekufa. Washirika hao wa Marekani wa karibu ni nchi za Israel, Uingereza, Ufaransa, Canada, Italia na nyinginezo za Ulaya. Raia wa nchi hizo wamekuwa wakitembelea mataifa mbalimbali duniani na Bara Afrika, ikiwemo Tanzania, kwa shughuli za utalii au miradi ya maendeleo.Misime aliwataka wageni hao, kutambua kuwa wapo salama, na aliwataka waendelee na shughuli za kila siku za maendeleo zilizowaleta. Aliwataka watalii kuendelea kutalii na wengine kuendelea kuja nchini kama kawaida.Alisema“Jeshi la Polisi lipo timamu na litaendelea kuimarisha ulinzi wa wananchi wake na wasiokuwa raia pia, watalii waendelee kuwa na amani na jeshi litakabiliana na kila anayetaka kuhatarisha usalama”.Kauli hiyo ya Misime imekuja siku chache, baada ya Ubalozi wa Marekani nchini kutoa taarifa ya kuwataka raia wake, kuongeza umakini katika kuhakikisha ulinzi wa usalama wao kutokana na vitisho hivyo, vilivyotolewa na magaidi. Ubalozi huo uliwataka raia wake, kutembelea tovuti ya ubalozi huo kila wakati, ili kupata taarifa za mara kwa mara kuhusu hali ya usalama.Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alibainisha kuwa askari wake, wapo kila kona ya mkoa huo, hasa kwenye maeneo ambayo yanatembelewa kwa wingi na mara kwa mara na raia wa nje, hasa wa kutoka Bara la Ulaya.
3
Hayo yalisemwa na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Ahmed Nassor Mazrui wakati akizungumza na wafanyabiashara wanaojishughulisha na bidhaa mbali mbali za vyakula katika maonesho ya biashara huko Maisara.Maonesho ya biashara yalifunguliwa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein yakitoa fursa ya wafanyabiashara wapatao 100 kushiriki na kuonesha bidhaa zao mbalimbali.Alisema uamuzi wa Serikali kupunguza ushuru kwa bidhaa muhimu za vyakula lengo lake kubwa kuhakikisha kwamba wananchi wanamudu gharama za kununua bidhaa hizo.“Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inawahakikishia wananchi wake kupunguza bei ya bidhaa muhimu za vyakula kwa ajili ya kutoa nafuu kwa wananchi kuwapunguzia makali ya maisha,” alisema.Alisema katika siku za hivi karibuni baadhi ya wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu wamekuwa wakipandisha bei ya bidhaa za vyakula bila ya sababu za msingi wakati tayari bidhaa hizo ushuru wake umepunguzwa.Alisisitiza na kusema Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria wafanyabiashara wa aina hiyo ambao wamekuwa wakipuuza masharti na makubaliano yaliyowekwa kwa wafanyabiashara wakubwa waagizaji wa bidhaa muhimu.Kwa muda mrefu Serikali imejenga utamaduni wa kupunguza kodi kwa bidhaa zinazoingizwa nchini ikiwemo sukari unga wa ngano pamoja na mchele ili kutoa unafuu kwa walaji.Salum Juma Ahmed wa kampuni ya kuagiza bidhaa za mchele nje ya nchi, alikiri kuwepo kwa tatizo la baadhi ya wafanyabiashara wanaonunua bidhaa kwao kuzipandisha bei kinyume na utaratibu.“Ni kweli wapo wafanyabiashara wanapandisha bei ya bidhaa za vyakula kiholela kinyume na sheria na kuwasababisha ugumu wa maisha,” alisema.Aidha baadhi ya wananchi wa kisiwa cha Pemba wamekuwa na malalamiko kama hayo ambapo bidhaa zinapofika huko bei yake inakuwa tofauti na ile ya Unguja.
5
RAIS wa Rwanda, Paul Kagame ameushangaza ulimwengu baada ya kuwaachia huru wafungwa 2,140 walioomba msamaha, ikiwa ni pamoja na wanasiasa maarufu nchini humo.Hatua hiyo imepongezwa na wanasiasa walioachiwa huru na imeleta furaha kubwa katika taifa hilo la Afrika Mashariki, kwa kuonesha mwelekeo mpya wa kisiasa na kidemokrasia.Miongoni mwa wafungwa walioachiwa huru ni Victoire Ingabire, ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Force Democratique Unies du Rwanda (FDI).Ingabire alihukumiwa miaka 15 jela tangu mwaka 2010. Mwingine ni mwanamuziki, Kizito Mihigo ambae alikuwa amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela.Ingabire aliyefungwa mwaka 2010, alikutwa na hatia ya kufanya uchochezi kwa wananchi ili kuiasi serikali na kuunda makundi ya silaha ili kuivuruga nchi na kupuuza mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya watutsi.Aahidi kumsaidia Kagame kuijenga Rwanda Baada ya kuachiwa huru, Ingabire alimshukuru Rais Kagame na kusema kuanzia sasa ndio mwanzo wa uhuru wa kisiasa na demokrasia ya kweli nchini Rwanda.Alisema kutokana na nia nzuri ya rais ya kujenga nchi, yuko tayari kumuunga mkono katika kuiletea maendeleo Rwanda."Nina furaha kwa hatua iliyochukuliwa na rais, sasa nitarejea kuendelea na maisha kama kawaida na kusaidia maendeleo ya nchi,” alisema Ingabire."Nimekuwa nikifuatilia nikiwa gerezani hali ya mambo inavyoendelea nchini, kuna mafanikio mengi yaliyofikiwa, na ninadhani tunaweza kupiga hatua zaidi tukishirikiana pamoja kwa sababu kuna mengi ya kufanya. Hii ndiyo njia nzuri ya kujenga nchi yetu kwa kuheshimu mawazo ya wale tunaohisi ni wapinzani, nampongeza rais ambaye ameamua kunipa msamaha na kutoka nje ya gereza,” aliongeza Ingabire.Tangu wakati huo, kumekuwa na shinikizo la kumtaka Rais Kagame kumwachia huru. Hatua ya serikali kumwachia huru, inatajwa kuwa hatua muhimu kuchukuliwa na utawala wa Rais Paul Kagame, ambaye anaongoza taifa hilo la Afrika Mashariki kwa muhula wa tatu sasa.Februari 2015 mwanamuziki Kizito Mihigo alihukumiwa miaka 10 gerezani baada ya kukiri kuhusika na uhalifu, ikiwa ni pamoja na njama ya kumuua Rais Paul Kagame na viongozi wengine wa nchi.Mwanasiasa mwingine aliyeachiwa huru mwishoni mwa wiki ni aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa FDI, ambaye naye pia alimshukuru Rais Kagame kutokana na hatua ya kijasiri na ya kizalendo.Alisema pamoja na kwamba hatua hiyo imechochewa na shinikizo linaloendelea kimataifa hasa wakati huu ambapo Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Louise Mushikiwabo akiwania nafasi ya kuwa katibu mkuu wa shirika la nchi zinazozungumza Kifaransa.Katibu Mkuu katika serikali ya Rwanda anayehusika na mambo ya nje, Olivier Nduhungirehe alisema hatua hiyo imekuja kutokana na ombi la wahusika wenyewe, kumuandikia rais mara kadhaa wakimuomba msamaha ;na sio vinginevyo.
3
Na JOSEPH SHALUWA MFALME wa Pop duniani, hayati Michael Jackson ‘MJ’ alifariki dunia Juni 25, 2009. Ndoto zake zote zilizimikia hapo. Chanzo cha kifo chake kinaelezwa ni kuugua, pamoja na maradhi mengine MJ alikuwa akikabiliwa na msongo wa mawazo na matatizo ya kisaikolojia yaliyopelekea kupatwa pia tatizo la akili. Lakini nyuma ya pazia inadaiwa kuwa, MJ alifariki baada ya kuzidisha kipimo cha dawa za kulevya wakati akiwa katika hali ya ugonjwa huku akitumia dawa maalum za kutuliza maumivu makali. Maelezo ya daktari wake binafsi, Dk. Conrad Murray yanafafanua kuwa MJ alikuwa katika hali ya kukosa usingizi, iliyosababishwa na madawa makali ya kuzuia maumivu makali aliyokuwa akiyapata siku 60 za mwisho wa uhai wake. Hata hivyo, maelezo mengine ya Dk. Murray yanaeleza kuwa matumizi ya dawa za kulevya ni sababu nyingine iliyochangia kifo cha staa huyo mwenye rekodi ya ajabu kwenye muziki wa Pop duniani. Tuachane na Michael Jackson. Hapa nchini wapo mastaa kadhaa ambao maisha yao yameharibika kabisa mara baada ya kutopea kwenye matumizi ya dawa za kulevya. Wapo wengine waliodaiwa kufariki kutokana na kuathirika vibaya na dawa hizo. Kila mtu anasema lake, lakini ukweli ni kwamba dawa za kulevya ni hatari kwa maisha ya binadamu. Kuna waliokuwa wanamuziki wakali kabisa, wenye sauti tamu lakini mara walipogusa tu dawa za kulevya vipaji vyao vikaporomoka na ukawa mwisho wao. Wengine leo hii wanajaribu kuibuka tena. Rehema Chalamika ‘Ray C’ anaweza kuwa mfano mzuri. Kama mfano huo hautoshi, yupo Chid Benz. Yule mwenye sauti tamu, nzito, inayosisimua. Leo yuko wapi? Naye anadaiwa tatizo ni madude. Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitaja orodha ya watu wanaotuhumiwa kwa matumizi na usambazaji wa dawa za kulevya. Walitajwa wengi wakiwemo wanasiasa, wafanyabiashara na wasanii. Kati ya wasanii waliotajwa ni pamoja na staa wa kunogesha video za wasanii, Agnes Gerald ‘Masogange’, mwigizaji Wema Sepetu, Mbongo Fleva Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, Khaleed Mohamed ‘T.I.D’ na wengine. Mashauri ya baadhi ya watuhumiwa hao yanaendelea mahakamani. Lakini nataka kuzungumza kidogo na jamii ya wasanii wa Bongo kuhusiana na matumizi na usambazaji wa dawa za kulevya.   Ipo mifano mingi inayoonyesha madhara ya moja kwa moja ya kutumia au kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.   UTUMIAJI Athari za dawa za kulevya zipo wazi kabisa, hakuna aliyeingia kwenye utumiaji akapata matokeo chanya. Ni kujidanganya kwamba eti kwa kutumia mihadarati utapata stimu zaidi za kufanya vizuri kwenye sanaa. Zaidi waliotumia tunawaona sasa hivi wakiwa kwenye mateso makubwa. Wamepoteza uwezo wao kisanii, wamekuwa wagomvi, wengine wamepoteza haiba zao na wamedhoofu kabisa miili yao. Kwa sasa wamekuwa tegemezi na zaidi wanatafuta tiba za kukabiliana na kuacha matumizi ya madawa hayo. Kumbuka kuingia ni rahisi sana, lakini kuacha ni mzigo mzito. Ni afadhali ambaye hajawahi kutumia, akaachana kabisa na wazo hilo. Hakuna cha maana atakachopata zaidi na majuto. Kama hujawahi, kaa mbali – usithubutu kabisa.   USAMBAZAJI Kila mmoja anaelewa kinachompata mtu anayekutwa na hatia ya kusambaza dawa za kulevya. Ni kifungo jela. Maana yake ndoto zako zote zinazimika mara moja. Wapo Watanzania kadhaa ambao wamekamatwa nje ya nchi na wanatumikia vifungo vyao hukohuko kutokana na kukutwa na dawa za kulevya. Kimsingi athari ni kubwa, maana ukiachana na hiyo, wale wanaotumiwa kama punda kwa kumezeshwa dawa hizo na kusafiri nayo, kuna matatizo makubwa kiafya yanayoweza kumkuta mhusika ikiwemo kifo.   UJANJA NI NINI? Vijana wa sasa wanaamini ujanja ni pesa. Yaani mtu akishakuwa na fedha za kutosha, basi kunakuwa hakuna mjanja kama yeye. Ni kweli. Fedha ni kila kitu, lakini si kila njia ya kupata fedha ni salama. Achana na shotikati. Ujanja ni ubunifu. Lazima kijana uwe mbunifu, ufikirie nini ufanye ili uweze kufanikiwa kifedha. Kama ni mwanamuziki imba zaidi. Toa tungo kali, utatoboa. Kama ni msanii tafuta watu wenye mawazo mazuri ya hadithi, chagua wasanii wenye vipaji, wekeni kambi. Mkitoka mtakuwa na sinema nzuri ya kusisimua ambayo inaweza kubadili maisha yako. Siyo kuhangaika na madude!
1
Na TUNU NASSOR -DAR ES SALAAM WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inakusudia kupeleka muswada bungeni utakaowabana madereva wa pikipiki za kubeba abiria, maarufu bodaboda kuwa na bima ya afya kabla ya kupewa leseni ya kutoa huduma kutokana na ongezeko la ajali. Akizugumza Dar es Salaam jana wakati wa ufunguzi wa kambi ya utoaji wa miguu bandia kwa watu 600 katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema sababu ya kusudio hilo ni wingi wa ajali zitokanazo na bodaboda na kuongeza mzigo wa gharama za matibabu kwa sekta ya afya. Ummy alisema taasisi hiyo kwa mwezi imekuwa ikipokea majeruhi 700 hadi 900 wa ajali za barabarani, idadi ambayo imekuwa ikiongezeka kila siku. Alisema awali kabla ya kuruhusu pikipiki kuwa chombo cha usafirishaji wa abiria, MOI ilikuwa ikipokea majeruhi wa ajali 400 hadi 600 kwa mwezi. “Nimeongea na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na kumwomba watafute jinsi ya kudhibiti pikipiki hizo, kwani zimekuwa zikibeba zaidi ya abiria wawili hadi watatu, nimemuomba kabla dereva bodaboda hajapewa leseni, sharti la kwanza awe na bima ya afya ndio apatiwe leseni ya udereva,” alisema Ummy. Alisema bima ya afya ni muhimu kwa sababu gharama za matibabu mtu anapopata ajali ni kubwa na zinaongeza mzigo katika sekta hiyo. “Gharama za upasuaji mdogo katika Taasisi ya MOI ni Sh 200,000 na kupatiwa mguu bandia inagharimu Sh milioni 1.5 hadi 3 jambo ambalo ni mzigo mkubwa kwa sekta ya afya,” alisema Ummy. Aidha alisema kambi ya upimaji wa watu wanaotakiwa kupatiwa miguu bandia, waliojiandikisha walikuwa 900 na waliofanikiwa kupewa miguu hiyo ni 600, hivyo ameahidi kutafuta njia nyingine ya kuwapatia miguu hiyo watu 300 waliobaki. “Tumefanikiwa hili kwa kushirikiana na Ubalozi wa India ambao umekuwa mstari wa mbele kuchangia sekta ya afya, ambapo mwaka jana walichangia dawa zilizokuwa na thamani ya Sh bilioni mbili na wameahidi tena kutoa fedha hizo mwaka huu, ambapo dawa za Sh milioni 500 watapewa MOI,” alisema. Alisema ameona dawa za Sh milioni 500 wapewe MOI kwa sababu amekuwa akiridhika na huduma zinazotolewa katika taasisi hiyo licha ya kuwa na baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo. Aidha Ummy aliwahakikishia MOI kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto zilizopo kwa wakati ili waendelee kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wananchi. Naye Mwenyekiti wa Bodi wa MOI, Charles Mkonyi aliishukuru Serikali kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma pamoja na kufunga vifaa vya kisasa vya uchunguzi. “Tunaomba kusaidiwa upanuzi wa eneo la mazoezi kwa sababu kwa sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wenye mahitaji hayo,” alisema.
0
Yanga itashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 iliyopata wiki iliyopita katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara wanahitaji sare au ushindi wowote kuwawawezesha kusonga mbele hatua ya makundi.Ikiwa watafanikiwa basi watajiwekea historia nyingine mpya baada ya mwaka uliopita kufanikiwa kuishia hatua hiyo.Kikosi hicho kitamkosa mchezaji tegemeo Obrey Chirwa ambaye alibaki Dar es Salaam kutokana na matatizo yake na klabu.Lakini pengine uwepo wa Donald Ngoma, Amis Tambwe, Thaban Kamusoko, Haruna Niyonzima kwa kushirikiana na wengine ukasaidia timu hiyo kusonga mbele.Yanga imekuwa na utofauti mkubwa katika mechi za ugenini licha ya kupoteza mara nyingi, lakini imekuwa ikicheza mchezo wa nguvu kuliko inavyokuwa nyumbani japokuwa imekuwa haisaidii.Wanakutana na MC Alger ambayo imekuwa ikijitahidi katika michezo ya nyumbani kufanya vizuri.Katika michezo iliyopita timu hiyo ya Algeria ilifungwa 2-1 dhidi ya Benchem United ya Ghana kisha nyumbani kwao katika mchezo wa marudiano wakashinda 4-1.Aidha, walifungwa mabao 2-1 ugenini na nyumbani kwao wakashinda 2-0 dhidi ya Renaisance hiyo yote ikiwa ni michezo ya awali ya michuano hiyo ya Shirikisho.Kwa kuangalia mechi hizo inaonyesha wazi kuwa ni timu yenye nguvu hasa inapokuwa mbele ya mashabiki wake kwenye uwanja wao wa nyumbani.Lakini pia, kwa kuangalia mchezo dhidi ya Yanga walikuwa wakicheza kwa kujilinda zaidi wakiamini kwamba kila kitu watamaliza kwao.Wachezaji wa kuogopwa ni Awady Said, Goveri Kaled na Nekkache Hichem, ambao wanaonekana nmi hatari zaidi.Yanga iliondoka juzi kwenda Algeria huku kocha wake msaidizi Juma Mwambusi akit- amba kuwa wanakwenda kumalizia kazi na kuwataka mashabiki wa timu hiyo na Watanzania kwa ujumla kuwa watulivu.
4
ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa Azam, Hans Van Der Pluijm amesema kwa sasa hana haraka anarudi nyumbani Ghana kujadiliana na familia yake kuhusu yaliyotokea.Pluijm amesema hayo siku chache baada ya kufukuzwa kazi katika kikosi cha Azam na aliyekuwa msaidizi wake Juma Mwambusi, baada ya kupata matokeo mabaya takriban mechi tatu mfululizo kwenye Ligi Kuu Bara.Pluijm amesema, kwa sasa hajapata ofa ya kwenda kuitumikia timu yoyote na hana haraka ya kutafuta timu na kwamba anarudi baada ya kuitwa na familia yake.“Naenda nyumbani Ghana kujadiliana na familia yangu kuhusu yaliyotokea baada ya kufukuzwa kazi, baada ya hapo nitasema kama nimepata timu mpya ya kufundisha au la,” alisema.Kwa sasa kocha huyo yupo nchini anaandaa mipango ya safari kurudi kwake Machi 10, mwaka huu.Mholanzi huyo amekiacha kikosi hicho kikiwa kwenye nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu baada ya kufikisha pointi 50.Hata hivyo, pamoja na Azam kumtimua kocha huyo hana rekodi mbaya kwani tangu amejiunga nayo msimu huu ameshaipa mataji mawili, kombe la Kagame na kombe la Mapinduzi.Kwa sasa kikosi hicho cha wanalambalamba kipo chini ya makocha wa timu zao za vijana, Abdul Mingange na Iddi Cheche watakaokiongoza kwa muda.Pluijm alitua Azam akitokea Singida United aliyojiunga nayo baada ya kuachana na Yanga aliyoinoa kwa mafanikio makubwa.
4
SERIKALI kisiwa cha Songosongo imetakiwa kushirikisha wananchi katika kuibua na kubuni miradi ya kimkakati ambayo itakujwa endelevu katika kusaidia, kuanzisha na kupanua wigo wa vyanzo vipya vya mapato katika kisiwa hicho. Kisiwa hicho kipo katika wilaya ya Kilwa na maarufu sana kwa uchimbaji wa gesi na uvuvi wa samaki wakiwemo pweza.Akizungumza katika ufunguzi wa jukwaa la pili kla wadau wa sekta ya uzinduaji wa gesi asilia na mafuta kata ya Songosongo, Diwani wa kata hiyo Said Mwinyi alisema kitendo cha kisiwa hicho kuendelea kutegemea mrabaha wa asilimia 20 kutoka wilaya hautoi sura ya mbele ya kisiwa hicho wakati gesi itakapokuwa imekoma.Alisema pamoja na Mtandao wa Mashirika yasiyo ya kiserikali mkoa wa Lindi (LANGO) kuwezesha uwapo wa majukwaa hayo ambayo yamesaidia kutoa elimu wakati umefika kwa wananchi na serikali kuibua miradi mipya ili kisiwa kuwa na uhakika wa kipato cha mtu mmoja na jamii.Lango limeendesha majukwaa hayo kwa ufadhili wa Shirika la Open Society Initiatives For Eastern Africa (OSIEA) na moja ya mafanikio ni kuwezesha wananchi wa Songosongo kupata haki yao ya mrabaha kutoka halmashauri ya wilaya ya Kilwa, mrabaha ambao wamesema unawasaidia kurekebisha hali ya mapato na matumizi ya serikali kisiwani hapo.Majukwaa hayo ambayo yanakuwa eneo huru la kuulizana maswali kati ya wananchi na taasisi zinaozohusika na sekta ya uziduaji kisiwani Songosongo,yamelenga kuimarisha ushiriki wa wananchi, uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa mapato ya tozo ya huduma katika sekta ya uziduaji wa gesi asilia na mafuta.Diwani Mwinyi alisema mradi huo wa mwaka mmoja sasa umewezesha wananchi kuelewa masuala mbalimbali kuhusu sekta ya uziduaji na namna ambavyo sekta hiyo inachangia maendeleo na kuona tozo ya huduma ya kutoka halmashauri ya Kilwa inayosababishwa na gawio la asilimia 20 linavyofanyakazi katika kisiwa hicho.Alisema mafunzo yaliyotolewa na LANGO na kuwezeshwa kuundwa kwa majukwaa yamewezesha wananchi kuona na kuibua fursa mbalimbali zinazoambatana na sekta ya uziduaji gesi asilia na mafuta .Aidha kwa sasa wananchi wanaweza kuhoji fedha zao na kuona namna bora ya kuweza kuwekeza kwa manufaa ya vizazi vijavyo. Katika jukwaa hilo Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Songosongo Hamza Hamza alisema kutokana na mafundisho na msaada wa LANGO, wameweza kubaini na kufuatilia halmashauri ya Kilwa ya tozo ya huduma kwa kijiji hicho yenye thamani ya sh milioni 254.Alisema halmashauri ya wilaya ya Kilwa ambayo ‘ilijikopesha’ fedha hizo za kuanzia mwaka 2014 hadi 2018 kwa sasa imelipa kwa mikupuo miwili jumla ya Sh milioni 116 na kubakiza Sh milioni 138. Aidha Ofisa mtendaji huyo alisema kwamba Sh 29,800,000 kati ya fedha hizo, zimetumika kulipa posho ya walimu wanne wa kujitolea, posho kwa walinzi na kuchangia fedha za kambi ya darasa la saba na kidato cha nne mwaka huu.
3
BODI ya Uratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali imetakiwa kuhakikisha miradi inayotekelezwa na mashirika hayo inazingatia mipango na vipaumbele vya serikali na wananchi katika eneo husika.Hayo yameleezwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile wakati wa kufunga mafunzo ya wajumbe wa bodi hiyo yaliyofanyika jijini hapa.Alisema ili kusaidia utekelezaji wa pamoja wa afua mbalimbali na hivyo kuharakisha juhudi za kuwaletea maendeleo ya wananchi wa Tanzania, ni lazima bodi kuzingatia kwa umakini vipaumbele na mahitaji ya wananchi na serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.“Katika eneo la kisheria ambalo napenda bodi izingatie kwa umakini ni eneo la vipaumbele na mahitaji ya wananchi na serikali katika kutekaleza miradi ya maendeleo,” alisema na kuongeza: “Kwa kuimarisha uratibu, serikali itaweza kuwa na utambuzi wa maeneo yenye uhitaji wa huduma za kijamii, hivyo kupunguza mrudikano wa shughuli za NGOs katika eneo moja na kuacha maeneo mengine yenye uhitaji mkubwa wa huduma za jamii”.Alisema uratibu imara utaiwezesha serikali kujipima na kutathimini utekelezaji wa mipango na mikakati yake ya maendeleo kwa kuhusisha juhudi zilizofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali, jambo ambalo litawezesha serikali kutumia rasilimali za umma kwa ufanisi kwa kuandaa bajeti inayozingatia mahitaji halisi ya wananchi. Bodi hiyo mpya ambayo ni ya nne chini ya uwenyekiti wa Dk Richard Sambaige imepewa mafunzo ya kuwajengea uwezo katika sheria juu ya miongozo ya uendeshaji wa NGOs nchini.Naye, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk John Jingu alisema kuanza kazi kwa bodi mpya hiyo kutasaidia mabadiliko chanya kwenye sekta ya NGOs nchini hasa katika suala zima la uwazi na uwajibikaji kwa wananchi wanaowahudumia. Naye, Kaimu Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Neema Mwanga alisema baada ya kuzinduliwa kwa bodi hiyo kutasaidia baadhi ya NGOs kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria, kanuni za uwazi na uwajibikaji kwani kinyume chake chombo hiki kitawachukulia hatua.
3
BEIJING, CHINA SERIKALI ya China imesema itaziwekea ongezeko la asilimia 25 la ushuru bidhaa zinazoagizwa kutoka Marekani zenye thamani ya dola bilioni 60 kuanzia Juni mosi. Baraza la Ushuru na Forodha la nchi hiyo limesema hatua hiyo ni jibu kwa tangazo la Marekani la kuziongezea asilimia kama hiyo bidhaa za China zenye thamani ya dola bilioni 200. Utawala wa Rais Donald Trump umewaagiza maofisa wa biashara kutambua aina nyingine za bidhaa kutoka China zenye thamani ya dola bilioni 300 ili ziwekewe pia vikwazo vya ushuru. Mazungumzo ambayo yamekuwa yakifanyika baina ya nchi hizo mbili zinazoongoza kiuchumi duniani kutafuta makubaliano ya kibiashara, yalivunjika Ijumaa iliyopita bila kufikiwa mwafaka. Saa moja kabla ya China kutangaza ongezeko hilo la ushuru, Rais Trump alikuwa ameionya kutothubutu kulipa kisasi, la sivyo hali itakuwa mbaya zaidi. Lakini Wizara ya Mambo ya Nje ya China ilijibu kuwa nchi hiyo kamwe haitasalimu amri kwa shinikizo litokalo nje.                                                                                                                                   
2
Na ARODIA PETER DODOMA SERIKALI iko mbioni kukamilisha muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote na kuuwasilisha bungeni Septemba. Pia wizara hiyo ipo katika maandalizi ya muswada wa marekebisho ya Sheria ya VVU na Ukimwi sura Na 431 ili kuruhusu watu kujipima wenyewe na kushusha umri wa mtu kupima bila ridhaa ya mzazi au mlezi kutoka miaka 18 hadi 15.  Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akisoma bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2019/20 bungeni jana, alisema maandalizi ya mpango huo yamekamilika ikiwamo mkutano wa kuelimisha wabunge kuhusu mkakati wa uboreshaji mfumo wa ugharamiaji wa bima  za afya. Katika maandalizi hayo, alisema wabunge 19 walifanya ziara nchini Rwanda na Ghana Disemba mwaka jana kwa lengo la kupata uzoefu wa namna nchi hizo zilivyoweza kutekeleza mfumo huo wa bima kwa wote. Katika hotuba hiyo, waziri Ummy alitaja vipaumbele vya wizara hiyo kwa mwaka 2019/20 kuwa ni pamoja na kuendelea kununua na kusambaza chanjo kulingana na mahitaji, kuwakinga watoto wa umri chini ya mwaka mmoja na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo ambapo Sh bilioni 30 zimetengwa. “Wizara itaendelea kutekeleza afua mbalimbali za huduma ya kinga ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo vya kina mama vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto. “Kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kama vile kisukari, moyo, shinikizo la damu, saratani na magonjwa sugu kama vile pumu. Kuhusu ukimwi, Ummy alisema huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na maambukizi na VVU zimeendelea kutolewa na idadi ya watu wanaotumia dawa ya kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi imeongezeka kufikia wati 1,103,016 mwa Machi. Alisema pia wizara yale kwa kushirikiana ile ya Viwanda na Biashara na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Bohari ya Dawa imeandaa mwongozo unaoainisha fursa mbalimbali za uwekezaji katika viwanda vya dawa na vifaa tiba. Mwongozo huo utarahisisha upatikanaji wa taarifa katika uwekezaji wa viwanda vya dawa nchini ambapo hadi kufikia Machi mwaka huu viwanda nane vya dawa vinaendelea kujengwa nchini. Aidha Ummy alisema wizara yake imeendelea kuimarisha huduma za matibabu ya kibingwa kuokoa maisha ya wananchi wengine kupunguza idadi ya wagonjwa wanaopewa rufaa ya matibabu nje ya nchi.
3
Na SHARIFA MMASI-DAR ES SALAAM UNAUKUMBUKA ule msemo wa Kiswahili usemao ukitaka kazi ya jeshi lazima ugangamale? Kumbe msemo huo sio jeshini tu, hata kwenye mchezo wa gofu kwasababu bila nidhamu na kujituma mambo yanakuwa magumu. Kwa siku za hivi karibuni, gofu imekua miongoni mwa michezo inayoendelea kujizolea mashabiki wa kila rika. Ukiacha watu wazima ambao wamekuwa wakiutumia mchezo huo kama sehemu ya kulinda afya za miili yao, lakini pia kumekuwa na ongezeko la chipukizi wanaojitokeza kutaka kujifunza mchezo huo. Ongezeko la wachezaji hao wachanga wanaojifunza mchezo huo limekuwa likiwapa kazi kubwa makocha katika kufikia malengo kutokana na changamoto mbalimbali wanazopitia. MTANZANIA lilifanya mahojiano na kocha wa watoto chini ya umri wa miaka 18 katika klabu ya Gofu ya Lugalo iliyopo jijini Dar es Salaam, Athuman Chiundu, aliyezungumzia mambo mbalimbali yanayohusiana na mchezo huo. Chiundu anasema alianza rasmi kufundisha watoto kucheza gofu katika klabu ya Lugalo mwaka 2015 huku akiwa na jumla ya wachezaji tisa; wavulana watano na wasichana wanne. “Mwaka 2015 ndio nilianza rasmi kufundisha watoto mchezo wa gofu katika klabu ya Lugalo, kipindi naanza nilikuwa na watoto tisa tu, wanawake walikuwa wapo wanne na waliobaki ni wanaume. Chiundu anasema klabu hiyo kwa sasa ina jumla ya wachezaji 36 anaoendelea kuwapa mafunzo hadi watakapofikia hatua ya kupanda daraja na kupewa kibali cha kuwa wachezaji wa kulipwa (professionals). “Kwa sasa nina jumla ya wachezaji 36 ninaowanoa ambapo mipango yangu mikubwa ni kuhakikisha wote kwa pamoja wanafikia hatua ya kuwa wachezaji wa kulipwa kama nilivyo mimi mwalimu wao. Anasema changamoto kubwa anayokumbana nayo kwa watoto anaowafundisha ni uhaba wa vifaa na hiyo ni kutokana na kuwategemea wadhamini mbalimbali. “Vifaa ni moja ya changamoto kubwa inayoendelea kuniumiza kichwa mimi kama mwalimu wao, kama mnavyojua tabia za watoto kuna wakati wanafurahi wakijiona wamependeza na jezi zao za kufanana kipindi cha mazoezi lakini kwa sasa hilo ni tatizo kwetu. “Mipira ya kuchezea pamoja na fimbo zake ni janga kwa baadhi ya wachezaji, gharama zake ndiyo zinapelekea wazazi kushindwa kuwanunulia watoto wao na hii husababisha kugeuka ‘ombaomba’ kwa wenzao ambapo wakati mwingine husababisha kero. Akizungumzia suala la nidhamu kwa wachezaji anaowafundisha, anasema ni kitu kikubwa kinachotiliwa mkazo kuanzia uongozi wa juu wa klabu hiyo hadi yeye kocha mwenyewe. “Nidhamu ni kitu pekee kinachopewa mkazo ndani ya klabu ya Lugalo bila ya kujali rika ya mchezaji.” Chiundu anasema upande wake mchezaji yeyote mwenye utovu wa nidhamu, anampa adhabu ya kucheza kwenye viwanja vitatu ambapo atahitajika kupata alama nne katika kila kiwanja kimoja bila kukosea. “Moja ya adhabu ninayowapa wachezaji wangu pindi wanapokosea ni kuhakikisha wanacheza viwanja vitatu na kila kimoja atalazimika kupata alama nne na kama hatafanikisha zoezi hilo, atalazimika kupiga mipira 100 kutoka mita moja hadi 100 za kiwanja. “Ninapoona mchezaji kafanikisha hilo na bado nidhamu yake mbovu, sina budi kumfuta kabisa katika klabu yangu ili kuwa mfano wa wengine wenye tabia kama hiyo,” anasema Chiundu. Akizungumzia suala la maendeleo ya watoto hao, anasema yanaridhisha kwani hadi sasa wachezaji wawili wamefuzu vema kuchezea viwanja 18, huku akidai wakiendelea na mbio hizo, watapata kibali cha kuwa wachezaji wa kulipwa.
4
Mshambuliaji wa Yanga, Patrick Sibomana Jumamosi iliyopita aliweka rekodi mpya kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika ambayo inasimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf). Mshambuliaji huyo ambaye aliichezea Yanga mchezo wake wa kimataifa kwa kwanza kuanzia alipojiunga nayo akitokea Mukura ya Rwanda, amekuwa staa kwenye timu hiyo kuanzia alipojiunga nayo. Sibomana aliifungia Yanga bao lake wakati ilipotoka sare ya bao 1-1 na Township Rollers ya Botswana kwenye mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, Sibomana ambaye hadi sasa kwenye mchezo huo mmoja wa kimataifa na michezo ya kirafi ki aliyocheza ameshafunga mabao nane aliweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kwa msimu huu kufunga bao la penalti na wakati huohuo kukosa penalti kwenye Klabu Bingwa. Katika michezo yote ya awali iliyopigwa kuanzia Ijumaa hadi Jumapili, hakuna mchezaji ambaye aliweza kufanya jambo hilo la kufunga penati na kwenye mchezo huohuo kukosa penati. Hata hivyo, mbali na huyo pia Yanga iliweka rekodi ya kupata penalti mbili kwenye mchezo mmoja kati ya hiyo yote ya kimataifa iliyopigwa juzi.
4
Na Elizabeth Joachim,Dar es Salam TIMU ya soka ya Mtibwa Sugar ya Manungu mkoani Morogoro kuiwakilisha nchini katika mashindano ya Kuimataifa ya Shirikisho Afrika  mwakani baada ya kunyakua kombe la Shirikisho kwa ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Singida United. Mechi hiyo ya fainali iliyozikutanisha timu hizo zimepigwa katika uwanja Sheikh Amri  Abeid Karume uliopo mjini Arusha ambapo mtanange huo ulianza majira ya saa tisa. mapema dakika 22 ,  salum kihimbwa aliiandikia mtibwa bao la kuongoza, kabla ya issa rashidi kuongeza lingine dakika ya 37, lakini alikuwa ni salum chuku aliyeifungia bao la kwanza singida united dakika. dakika 71, kiungo wa singida united, tafadzwa kutinyu, aliisawazishia timu yake na kufanya ubao kusomeka 2-2, lakini dakika 81, rashid alipata kadi nyekundu kwa kumchezea rafu kiungo wa singida united, deus kaseke. winga  wa mtibwa sugar, ismail aidan, aliiandikia bao la tatu timu yake baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa kelvin kongwe na kufanya matokeo kuwa 3-2, na timu hiyo kuibuka na ushindi huo.
4
NA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM WAKATI mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu zimeshika kasi, hakuna dalili yoyote inayoonyesha kama mchezo kati ya Yanga dhidi ya Azam utakaochezwa Jumamosi Uwanja wa Taifa Dar es Salaam utatoa bingwa wa ligi hiyo. Yanga itaingia kwenye mchezo huo ikiwa inaongoza ligi kwa kuwa na pointi 46 sawa na Azam, ambayo inashikilia nafasi ya pili kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa huku Simba ikiwa nafasi ya tatu baada ya kujikusanyia pointi 45 katika mechi 20 ilizocheza. Yanga imefunga mabao 44 na kufungwa 9, huku Azam ikiwa imeziona nyavu za wapinzani wake mara 34 na kufungwa 11 kutokana na mechi 19 walizocheza ikiwa ni pointi moja nyuma ya Simba, ambayo imefunga mabao 35 na kufungwa 13. Pambano la Yanga dhidi ya Azam litachezwa huku timu zikiwa zimebakiwa na michezo 10 kila moja, wakati Simba imebakiwa na 9 ili kupatikana bingwa wa Ligi Kuu msimu huu. Michezo hiyo itakuwa na jumla ya pointi 30 ili timu iweze kuwa kwenye nafasi nzuri ya kujihakikishia ubingwa inatakiwa kunyakua zaidi ya pointi 15 hadi 18. Pointi hizo zinatokana na kuwapo kwa michezo 10, ambapo mitano kati ya hiyo inawezekana kutoa taswira halisi ya bingwa msimu huu. Yanga itacheza mechi 6 ugenini, huku 4 ikicheza katika uwanja wake wa nyumbani, Azam itacheza michezo mitano ikiwa kwenye dimba lake la Azam Complex na mingine mitano ikiwa ugenini, wakati Simba itacheza mechi 3 ugenini na mingine 6 ikiwa uwanja wake wa nyumbani. Moja ya mechi zinazoonekana kuwa ngumu kwa timu zilizopo kwenye nafasi tatu za juu ni ule utakaochezwa Aprili 2 kati ya Yanga na Kagera Sugar katika Uwanja wa Taifa, siku chache baadaye Azam itakutana na Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba. Presha itapanda zaidi Aprili 16 wakati Simba ikiikaribisha Azam kwenye Uwanja Taifa, Dar es Salaam, ambapo siku moja baadaye Yanga nao wataikaribisha Mgambo Shooting kwenye uwanja huo. Aidha, mchezo wa Machi 13 wa Simba dhidi ya Prisons utakuwa miongoni mwa michezo migumu ya mwishoni mwa msimu, ambayo inaweza kuwa na matokeo yasiyotarajiwa. Bingwa wa Ligi Kuu msimu huu anaweza kufikisha pointi 64 ambazo ni nyingi, ukilinganishwa na msimu uliopita wakati bingwa alikuwa na jumla ya pointi 55. Kutokana na hesabu hiyo, huenda bingwa wa msimu huu akapatikana baada ya michezo itakayochezwa kuanzia Aprili, ambapo timu nyingi zitakuwa zimefikia michezo kuanzia 25 na kubakiza mitano. Hatua hiyo inafanya nafasi ya ubingwa kuwa wazi kwa timu zote tatu zilizopo kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo. Kwa kuwa michezo iliyochezwa na timu za Ligi Kuu hadi sasa ni 20 kati ya 30, Yanga na Azam zitakuwa zikikamilisha hesabu hiyo huku zikiwa na viporo vya mchezo mmoja mkononi.
4
Na Mwandishi wetu -Zanzibar  WAZIRI wa Katiba na Sheria wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Khamis Juma Mwalim, ameitaka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kusimamia majukumu yao kwa ufanisi kama sheria na mwongozo inavyoelekeza. Akizungumza na ujumbe kutoka tume hiyo ofisini kwake Mazizini Unguja juzi, Mwalim alisema tume ina majukumu ya kuendeleza na kusimamia masuala ya haki na utawala bora nchini, ni vema ikasimamia kwa uadilifu zaidi. Shimo aliahidi wizara yake kuendelea kufanya kazi na tume hiyo kwa nguvu zote. Alisema wizara yake itahakikisha taratibu na miongozo inafuatwa katika kusimamia demokrasia, utawala bora na haki za binadamu chini ya utawala wa sheria. “Katiba, sheria, tume kwa upande mwingine ni watoto pacha, lazima tuungane pamoja kama mihimili ili kusimamia vema majukumu ya nchi na kuendeleza amani na mshikamano wa nchi yetu,” alsema Shimo. Naye Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Mathew Mwaimu alisema jukumu kubwa la tume hiyo ni kulinda, kutetea na kuhifadhi haki za binadamu nchini. Alisema katika kutekeleza jukumu hilo, tume inayo mamlaka ya kupokea malalamiko kwa njia mbalimbali na kuanzisha uchunguzi wake endapo itaona kuna uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Mathew alimhakikishia  Mgumba kuwa tume itafanya kazi kwa uadilifu na kutimiza wajibu wao kwa kuzingatia taratibu na kufuata Katiba na sheria za nchi. Kuhusu masuala ya haki za binadamu,  alisema tume hiyo ni sehemu muhimu inayosimamiwa na Wizara ya Katiba na Sheria. Alisema ushirikiano mkubwa wa kiutendaji unahitajika ndani ya wizara inayoshughulikia masuala ya utawala bora ili kupata taarifa sahihi. Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Nyanda Shuli alisema kupitia ushirikiano huo, atatatua changamoto zitakazojitokeza na kupatiwa ufumbuzi. Alisema tume haitaruhusu mwanya kwa baadhi ya vikundi ama taasisi kuhatarisha amani na kusababisha ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala bora.
3
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), George Simbachawene, ametoa siku 14 kwa watengenezaji na wasambazaji wa mifuko mbadala nchini kuhakikisha inakidhi vigezo vyote stahiki ikiwamo uwekaji wa nembo ya mmiliki au kampuni. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kufanya ziara katika Bandari ya Dar es Salaam jana, Simbachawene alisema wazalishaji wa mifuko mbadala ambao hawakidhi vigezo na masharti yaliyowekwa na mamlaka husika wanasababisha wazalishaji wa ndani kukosa soko na kupoteza mapato ya serikali.“Ni lazima tujue nani anazalisha na kusambaza mifuko hii mbadala, hawa wanaozalisha ndani na kufuata taratibu zote wanakosa soko kwa sababu ya wengine wanaofanya biashara hii kiholela bila kufuata taratibu,” alisema. Aidha, waziri huyo alisema msako mkali utafanyika na kwa yeyote atakayekutwa akizalisha au kuuza mifuko mbadala isiyokuwa na vigezo vilivyowekwa na mamlaka husika na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo kuchomwa moto mifuko hiyo.Simbachawene pia aliagiza watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kitengo cha Ukaguzi Bandarini kufanya kazi saa 24 kwa kushirikiana na watumishi wa taasisi nyingine za serikali ili kuongeza nguvu kazi katika ukaguzi wa mizigo inayoingia nchini. “Ufanisi wa bandari upo kwenye utoaji na uingizaji wa mizigo ndani na nje ya nchi. Ikibidi nguvu kazi iongezeke ila wawe ni wale wenye taaluma zinazoendana na kazi hii ili ifanyike kwa haraka na uhakika,” alisema. Alisema kanuni zimebainisha wazi kuwa, mtu yeyote anayeingiza nchini, anayesafirisha nje ya nchi au anayezalisha vifungashio vya plastiki ambavyo havijazuiwa na kanuni hizo, anatakiwa kuhakikisha kwamba vinakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Tangu serikali iweke katazo la utengenezaji, usambazaji na uuzaji wa mifuko ya plastiki mwezi Juni, mwaka huu, hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa kuhakikisha mifuko mbadala inatumika ili kutunza mazingira.
3
Kuna taarifa zinazodai kuwa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam (UDART) yamegoma na kusababisha usumbufu kwa wananchi.Leo saa mbili asubuhi kuna wananchi waliodai kuwa, walikuwa vituoni tangu saa tatu asubuhi na kwamba, hakukuwa na mabasi ya mwendokasi yaliyokuwa yakitoa huduma."Imekuwa kero sana, kwa hiyo nilikuwa naomba Serikali kwa jicho la tatu iangalie kama hawa watu biashara imewashinda waachieni wenye biashara hizi wanaoweza. Matajiri wapo wengi wanaotaka hizi biashara, au la warudishe hizi daladala"amesema mmoja wa wananchi aliyekuwa akisubiri usafiri Kimara.Inadaiwa kuwa, mabasi ya UDART yamekuwa machache hivyo yaliyopo yanapita kwenye vituo vingi yakiwa yamejaa na hayasimami.“Tumembeleza tumemwambia tunaomba utuletee gari moja tupu ameshindwa. Tunaomba ya menejimenti ya mtu wa UDART tumpigie sisi wenyewe tunajua wewe so mtu sahihi wa ku-complain (kulalamika), hatuna namba, namba zile pale zipo hamna hata moja inayopatikana, nimejaribu brother, hamna hata moja inayopatikana pale ambayo ni ya UDART” amesema mmoja wa wananchi kwenye kituo cha Kimara Korogwe.
3
Na FARAJA MASINDE -DAR ES SALAAM CHAMA cha Damokrasia na Maendeleo(Chadema), kimewaagiza wabunge wake kote nchini kuhoji iwapo kutakuwa na mswaada wa mabadiliko ya tume huru ya uchaguzi, ili Watanzania waweze kupata viongozi wanaowataka kuelekea uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Kauli hiyo ilitolewa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Chama hicho, John Mnyika, muda mfupi kabla ya kufanya kikao na wanachama wa chama hicho Jimbo la Kibamba, alisema kuwa kuna haja ya kufanyika mabadiliko ya tume ya uchaguzi ili kuepuka machafuko kama alivyoonya juzi Rais Dk. John Magufuli akiwa visiwani Zanzibar. Kauli ya Mnyika imekuja ikiwa ni siku moja tu imepita tangu, Rais Dk.  Magufuli alipowataka Wazanzibar kutorudia makosa yaliyojitokeza miaka ya nyuma, wakati wa Uchaguzi Mkuu. Mnyika alisema kuwa ni lazima kuwapo kwa tume huru ya uchaguzi ambayo itaenda sambamba na kuwapo kwa haki ya kupingwa kwa matokeo mahakamani pamoja na mgombea anayekuwa peke yake kupigiwa kura ya ndiyo na hapana. “Ni muhimu kuwa na tume huru ya uchaguzi, na kesho(leo) vikao vya Kamati za Bunge vinaanza, na Bunge rasmi Januri 28, kama tunavyofahamu kwamba tayari Rais Dk. Magufuli ameshasema kwamba hataki kuona yaliyotokeo Zanzibar yajirudie basi Watanzania wote, taasisi za dini ziombee hili, Asasi za kiraia ziwaunganishe Watanzania, na vyama vya Siasa vipiganie upatikani wa tume huru ya uchaguzi. “Na niwaombe wabunge wa Chadema kuwa mstari wa mbele katika hili wahakikishe kuwa kuanzia leo (jana) wimbo wetu unakuwa ni tume huru mpaka tupate tume huru ya uchaguzi,” alisemaMnyika.  “Hivyo, kama itafikia hadi Bunge linaanza Januri 28, kukiwa bado hakuna mswaada wowote kwa hati ya dharura ya marekebisho manne ya Katiba ambayo ni tume huru ya uchaguzi, kuruhusu matokeo ya urais kupingwa mahakamani, mgombea wa urais kuzidi asilimia 50 ya kura tofauti na sasa na mgombea anayepita peke yake kupigiwa kura ya ndiyo na hapana badala ya kupita bila  kupingwa kama ilivyo sasa. “Hayo yanahitajika ni lazima wabunge wetu wafuatilie kama kuna muswada kama huu na kama serikali haitafanya hivyo basi wabunge wa upinzani waungane watengeneze mswaada na waupeleke bungeni na kitakachotokea tutawaeleza Watanzania,” alisema Mnyika. Kuhusu kauli ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Dk. Bashiru Ally, ya kusema kwamba chama hicho kinashinda kwa kuwa kina wapiga kura wa kutosha, Mnyika alisema kuwa wao wanawanachama wa kuwachagua wa kutosha lakini wamekuwa wakiangushwa kutokana na kukosekana kwa tume huru. “Sisi tunawapiga kura wa kutosha ndiyo maana CCM wao wamekuwa wakitumia watendaji wa manispaa kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka jana kuengua wagombea wote wa chadema kwenye mitaa mbalimbali nchini. “Tayari, Mkutano Mkuu wa chama uliazimia kwamba tusitoe ushirikiano kwa viongozi wa serikali za mitaa waliopandikizwa katika maeneo mbalimbali, sasa nitoe agizo kwa chama kwamba ili tusitoe ushirikiano mkutano mkuu uliazimia kuwatangaza wale viongozi waliokuwa wameteuliwa na chama kugombea serikali za mitaa ndiyo watakuwa serikali vivuli kwenye mitaa mbalimbali. “Kwa hiyo vikao vianze ili kuweka mikakati ya kyuonyesha kwamba sisis tuna watu na wao wana dola mna tutawashinda,” alisema
3
habari za ndani ya klabu zinadai kuwa kiungo mkabaji wa Simba Mghana, James Kotei hana nafasi ya kuendelea kuichezea timu hiyo, hali ambayo imesababisha jina lake lianze kutajwa ndani ya Klabu ya Yanga kwa nia ya kumsajili. Mghana huyo ni kati ya wachezaji waliomaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu uliopita na inaelezwa kuwa uongozi wa Simba umepanga kuachana na kiungo huyo mkabaji anayemudu kucheza nafasi zote za ulinzi. Wachezaji wengine wanaotajwa kuachwa na Simba ni Muivory Coast, Zana Coulibaly, Mnyarwanda Haruna Niyonzima, Mganda Juuko Murshid na Waghana, Asante Kwasi na Nicholas Gyan. Azam FC imesisitiza kwamba, kipa anayetajwa kumalizana na Yanga, Metacha Mnata, ataitumikia Azam FC msimu ujao na wala haendi sehemu nyingine. Kauli ya Azam FC imekuja huku kukiwa na taarifa za Yanga kumalizana na kipa huyo ambaye yupo Misri na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwenye michuano ya Afcon. Metacha ambaye alikuwa kwa mkopo Mbao FC akitokea Azam FC, hivi sasa ni mchezaji huru kutokana na kumaliza mkataba ndani ya Azam FC. Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera ameutaka uongozi wa Yanga kuhakikisha unawabakisha wachezaji Raphael Daud, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Mrisho Ngassa ambao wote mikataba yao tayari imekwisha. Hata hivyo taarifa nyingine inasema kuwa klabu hiyo huenda ikaachana na kipa wao Mkongomani Klaus Kindoki.
4
Na Fredy Azzah-DODOMA LICHA ya kila Mbunge kulipwa posho ya Sh 220,000 kila anapohudhuria kikao cha Bunge, jana walikataa kukatwa Sh 30,000 za kumsaidia, Mshindi wa Tanzania super model, Asha Mabula, huku wengine wakitishia kwenda mahakamani endapo watakatwa fedha hizo.  Mshindi huyo anatarajiwa kushiriki shindano la dunia la World Miss Super Model litakalofanyika Macau, China. Tukio hilo lilitokea jana baada ya kipindi cha maswali na majibu.  Mbunge wa Urambo, Magreth Sitta, aliomba mwongozo kwa mwenyekiti wa kikao, Andrew Chenge, akiomba mrembo huyo achangiwe na wabunge angalau Sh 30,000 kila moja  zimsaidie anavyokwenda kuwakilisha Taifa. Maelezo hayo yaliibua minong’ono kwa wabunge, wengi wakipinga kukatwa fedha hizo. Wakati akijibu mwongozo huo, minong’ono iliendelea hatua iliyofanya Mwenyekiti wa Bunge, Chenge ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi, kuamua kutoa nafasi ya suala hilo kujadiliwa na wabunge. Aliyepewa nafasi ya kwanza alikuwa ni Mama Sitta, ambaye alisema anajua wabunge wana majukumu mengi, lakini yeye anataka  wachangie Sh 30,000 tu kwa sababu mrembo huyo anakwenda kuliwakilisha taifa. Alisema kitendo hicho siyo cha kwanza kwa vile  hata Serengeti Boys ilichangiwa na wabunge hao ilivyofuzu kwenda kwenye mashindano ya Afrika (AFCON) kwa vijana wa chini ya miaka 17. Mbunge wa Mafinga, Kosato Chumi, alisema jambo hilo ni jema kwa sababu anayechangiwa anakwenda kuliwakilisha taifa. Mbunge wa Viti Maalum, Martha Mlata (CCM),  alisema wabunge wanachangia sherehe mbalimbali zikiwamo za harusi, lakini anashangaa kukataa kumchangia mrembo huyo anayekwenda kuliwakilisha taifa. “Kwa hiyo nasema wanaotaka wachangie, wasiotaka waache,” alisema Mlata. Lakini Mbunge wa Nkasi, Ally Keissy, alisema kutoa mchango ni hiari ya mtu lakini yeye kwenye suala hilo hayupo tayari kutoa mchango wake. Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), alisema jimbo lake lina mambo mengi ya msingi ikiwa ni pamoja na wananchi wake kukabiliwa na baa la njaa ambalo serikali imekataa kulitambua. Alisema kwa sababu hiyo  suala la mrembo huyo ni vema likaachwa kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. “Hili jambo ni jema sana isipokuwa wananchi wangu wanakabiliwa na njaa sana, serikali imekataa kutoa chakula hivyo hili jambo hili ni vema akaachiwa Waziri anayehusika,” alisema Lissu. Mbunge wa Konde, Khatibu Said Haji (CUF), alisema yeye kwa imani ya dini yake mambo ya urembo yanakataliwa na ndiyo maana Zanzibar hayapo. “Wengine hata wakati anatambulishwa hapa tulijificha chini ya viti huku,” alisema. Baada ya wabunge hao kujadili, Chenge alisema kwa kuwa hoja hiyo imeshajadiliwa  atawahoji ni wangapi wanataka na wangapi wanapinga   kuchanga fedha hizo. Maelezo hayo yalipingwa na baadhi ya wabunge  huku  wengine wakiwa wanasema wapige kura na siyo kuhojiwa. Hata hivyo, Chenge aliwahoji na baadaye kuamua kwamba  waliokubali kukatwa fedha hizo wameshinda. Hatua hiyo ilifanya baadhi ya wabunge kuwasha vipaza sauti na kupinga hatua hiyo, huku Keissy akisema akikatwa fedha hizo atakwenda mahakamani. Taarifa ya Idara ya Habari Maelezo inasema kuwa, juzi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, alitembelewa na Mabula katika ofisi ya Wizara, Dodoma. Ilisema Mabula aliishukuru Serikali kwa kuwa karibu na tasnia hiyo kwa kushiriki kwenye mashindano yaliyofanyika Arusha mapema mwaka huu. Ilisema Mabula alimweleza Waziri kuhusu safari anayotarajia kuifanya ya kwenda  Macau kushiriki kwenye mashindano ya World Miss Super Model na kuiomba Serikali kumsaidia kupata wadhamini watakaochangia fedha za safari hiyo  aweze kuiwakilisha vema nchi kwenye mashindano hayo.
3
UONGOZI wa Kampuni ya Acacia kupitia Mgodi wa North Mara umezungumza na serikali kuelezea hatua zilizochukuliwa hadi sasa kudhibiti maji yenye sumu, ikiwa ni wiki moja tu ipite tangu Waziri wa Madini Doto Biteko, atangaze kufunga shuguli za mgodi huo endapo utashindwa kudhibiti maji ya sumu yanayotiririka kwenye makazi ya watu, ifi ke Machi 30, mwaka huu.Tamko hilo la serikali limeifanya kampuni ya Acacia kuchukua hatua za haraka za kudhibiti maji hayo ili kukwepa rungu la serikali la kuufunga mgodi huo. Machi 12, uongozi wa Acacia North Mara ulikutana na Waziri Biteko ofisini kwake jijini Dodoma kwa lengo la kueleza hatua iliyofikiwa ya kutekeleza agizo la serikali.Uongozi wa kampuni hiyo ukizungumza katika kikao hicho, ulieleza kuwa, tayari mgodi huo umechukua hatua za haraka tangu kutolewa kwa agizo na kwamba hadi sasa suala la kudhibiti maji yenye sumu limeshetekelezwa na hakuna maji yanayotiririka kuelekea kwenye makazi ya watu. Aidha, ulimweleza kuwa, pamoja na kudhibiti maji hayo kupitia bwawa la kuhifadhia maji yenye sumu yajulikanayo kitaalamu kama “topesumu” (Tailings Storage Facility- TSF) mgodi umeanza kuchukuwa hatua za kujenga TSF mpya.“Mhe. Waziri tumekuja kutoa mrejesho wa utekelezaji wa agizo lako, tunafurahi kukuambia kuwa tumetekeleza agizo hilo na kwa sasa hakuna maji yanayotiririka. Pamoja na hatua hiyo mgodi umeanza mchakato wa ujenzi wa bwawa jipya (TSF) la kuhifadhia topesumu,” walieleza. Pia ulimweleza Waziri Biteko kuhusu hujuma za uharibifu wa miundombinu ya bomba la maji yenye sumu unaofanywa kwa maksudi na wakazi wanaozunguka mgodi ili kufifisha juhudi zao za kudhibiti maji hayo wakiwa na lengo la kuufanya mgodi uonekane haujachukuwa hatua kudhibiti jambo hilo, ambapo walionesha picha mbalimbali ya namna bomba lilivyo pasuliwa ili maji yatiririke kuelekeka kwa wananchi.Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Biteko alieleza kuwa, amepokea taarifa ya kampuni husika na kuwapongeza kwa hatua zilizochukuliwa na kusema kuwa, ukweli wa jambo hilo atauthibitisha mara baada ya kupata ripoti ya wataalamu watakaokwenda kuhakikisha kuhusu utekelezaji wa agizo hilo na kuongeza,“katika hili sitanii juu ya kuufunga mgodi ikiwa utashindwa kudhibiti tope sumu”.“Naomba nirudie tena katika hili sitanii, sitabadilisha msimamo wangu kama serikali na utaendelea kubaki pale pale dawa pekee ni kutekelezwa kwa agizo hilo. Lakini niseme ukweli, nasikitishwa sana na kitendo hiki cha wananchi kupasua bomba, kwa hili sikubaliani nao na siwaungi mkono. Pia, aliongeza kuwa, atawasiliana na Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya kuona namna ya kudhibiti hali hiyo ili wale watakaobainika wachukuliwe hatua. Waziri Biteko alilitoa agizo hilo Machi 6, alipoutembelea mgodi huo hapo kwa ziara ya kikazi pamoja na kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Nyamongo wilaya ya Tarime.
3
Serikali imelieleza Bunge kuwa, waombaji 12,211 hawakupata mikopo kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu mwaka 2017/2018 kwa kuwa hawakukidhi vigezo na sifa zilizoainishwa kwenye sheria na mwongozo.Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya amesema, katika muda huo, wanafunzi 46, 131 waliomba mikopo na kwamba, maombi yao yalichambuliwa kwa kuzingatia Sheria ya Bodi ya Mikopo Sura 178 na Mwongozo wa Utoaji Mikopo kwa mwaka 2017/2018.Amesema, baada ya uchambuzi Serikali kupitia bodi ya mikopo ilitoa mikopo kwa wanafunzi 33,920 wa mwaka wa kwanza kwa kuwa walikidhi vigezo na sifa zilizoanishwa katika sheria na mwongozo uliotolewa 2017/2018.Kwa mujibu wa Manyanya, katika mwaka wa masomo 2017/2018 Serikali kupitia bodi ya mikopo iliandaa mwongozo wa utoaji mikopo uliotoa kipaumbele maalumu kwa yatima, wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu, na waliosoma sekondari au stashahada kwa kufadhiliwa.Ameyasema hayo jijini Dodoma wakati anajibu swali la Mbunge wa Chumbuni, ussi Salum Pondeza. Amejibu swali hilo kwa niaba ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kwa mujibu wa Mhandisi Manyanya, utaratibu na sifa za utoaji mikopo ya elimu ya juu unaongozwa na sheria iliyoanzisha Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Sura ya 178."Kwa mujibu wa sheria hii, mikopo ya elimu ya juu inapaswa kutolewa kwa Watanzania wahitaji na wenye sifa" amesema.Amewaeleza wabunge kuwa kifungu cha 17 cha sheria ya bodi ya mikopo kimetaja sifa kuu kuwa, mwombaji awe Mtanzania aliyedahiliwa katika taasisi ya elimu ya juu inayotambulika na Serikali, asiwe na vyanzo vingine vinavyogharamia masomo yake; na kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo wawe wamefaulu mitihani kuwawezesha kuendelea mwaka unaofuata.
3
WAKULIMA wa njegere wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wameiomba serikali kuwapiga marufuku madalali wa Dar es Salaam kuingia wilayani humo na kununua zao hilo, wakiwatuhumu kuporomosha bei.Badala yake, wakulima hao wameiomba serikali ifungue milango kwa wafanyabiashara kutoka Kenya waliowasifia kununua zao hilo kwa bei yenye tija.Katika mkutano wake na wananchi wa Kijiji cha Ukumbi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi ameelezwa na wakulima hao kwamba bei ya zao hilo imeporomoka mwaka huu kutoka Sh 50,000 hadi Sh 15,000 kwa gunia baada ya mwaka jana kuporomoka kutoka Sh 50,000 hadi 30,000.Mmoja wa wakulima hao, Expedito Saveli amesema kilimo cha zao hilo kimegeuka kilio kwa wananchi wengi wanaokitegemea kuendesha maisha yao. “Wakati Rais Magufuli akisisitiza ‘Hapa Kazi Tu’; kazi ya kilimo imekuwa haina msingi wa maana kwa wananchi wa kipato cha chini,” amesema mkulima mwingine, Thobadina Kigodi.Pamoja na njegere, Kigodi amesema madalali hao wamekuwa wakinunua gunia la mahindi la debe nane kwa Sh 30,000 badala ya Sh 70,000 walizokuwa wakiuza awali.“Hatutaki madalali wa Dar es Saalaam, tunataka Wakenya. Bei zao zinatupa matumaini ya kuendelea na kilimo hiki kwa kuwa kuna faida tunayopata na ambayo inatusaidia kwa mengi,”amesema.Hapi amemgeukia Ofisa Kilimo wa wilaya hiyo, Shehemba Kuzina akimtaka kujitafakari namna anavyoshughulikia kero za wakulima.“Ofisa kilimo lazima ujue bei za mazao katika wilaya yako. Kaa na viongozi wa vijiji, kata na wakulima wa wilaya yako mfahamishane taratibu za soko na masoko na bei zake,” amesema Hapi, baada ya ofisa kilimo huyo kukosa majibu ya taarifa muhimu za masoko ya mazao ya wilayani kwake.Hapi amepiga marufuku bidhaa za mazao hayo kuuzwa kwa lumbesa akisema utaratibu huo unamnyonya mkulima na kuwakatisha tamaa ya kuendelea na shughuli hiyo.Mbali na kutokuwa na taarifa za madalali hao wa Dar es Salaam, Ofisa Kilimo huyo alisema kuporomoka kwa bei ya njegere kumechangiwa na mikoa mingine ukiwemo wa Arusha kuongeza uzalishaji wake na kusababisha ushindani mkubwa katika soko.Hapi yupo wilayani Kilolo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya tarafa kwa tarafa katika wilaya zote za Mkoa wa Iringa akikagua shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wananchi kupitia kaulimbiu ya “Iringa Mpya.”
5
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM NAIBU Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Ukanda wa Nyanda ya Juu Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Jennifer Baarn, amemwomba Rais Dk. John Magufuli kuangalia kwa jicho la huruma ushoroba wa kituo hicho ili kufikia Tanzania ya viwanda. “Namuomba Rais Magufuli kusaidia shughuli za SAGCOT katika ushoroba wa Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania na hasa katika masuala ya miundombinu na shughuli za kongani. Vilevile asaidie watendaji wa Serikali ambao tunashirikiana nao katika kuinua kilimo nchini,” alisema Bi. Jennifer. Jennifer ambaye anamaliza muda wake katika nafasi hiyo, jana alifanya mazungumzo na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam na kusema kwamba, kitu pekee atakachokikumbuka kwa miaka sita aliyokaa Tanzania ni kufanya kazi na watu wanaopenda kujifunza na kuifikisha Tanzania juu kiuchumi. “Nitakumbuka vitu viwili, kwanza kufanya kazi. Tena kufanya kazi na watu wanaosoma kwa bidii ili kusaidia maendeleo ya nchi yao katika nyanda mbalimbali. Kingine nitakachokikumbuka ni Bagamoyo, naupenda mji ule mkongwe ambao ilikuwa kama nyumbani,” alisema Baarn. Aidha, mbali na mafanikio aliyoyapata kwa miaka sita aliyokuwemo kwenye kituo hicho kinachofanya kazi kwa ubia  kati ya sekta binafsi na sekta ya umma, Baarn alisema zipo changamoto kadhaa za kiutendaji ambazo zikipatiwa ufumbuzi, Tanzania itakuwa sehemu salama kwa chakula. Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey Kirenga, kwa namna alivyofanya naye kazi vizuri, Jennifer alisema hajawahi kumuona mtu anayejituma na kufanya kazi za kusaidia kilimo kukua kama yeye. SAGCOT inasimamia kilimo katika ukanda wa nyanda za juu kusini ambapo inagusia mikoa kadhaa kuanzia Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, Lindi na Mtwara pamoja na Ruvuma.
3
Iman Mketema –Dar es Salaam  Mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kilichopo Arusha, Meshack Daniel leo Desemba 1 amekabidhiwa kitita cha Shilingi milioni 226.8 baada ya kushinda mchezo wa Bahati Nasibu unaoendeshwa na kampuni mbili ya M-Bet na Perfect 12.   Meneja wa masoko wa M-bet, Allen Mushi, amemtangaza mshindi huyo huku akihamasisha watu wengine kucheza mchezo huo kwa kuwa wapo wengi walioshinda zaidi ya kiasi alichoshinda mwanafunzi huyo.   Mwanafunzi huyo amesema siku alipokwenda kubeti alitoka darasani kwao na kwenda kubeti kisha akarudi kuendelea na shughuli zake usiku akapokea meseji iliyomweleza ameshinda.   “Sikuwa na imani ya kushinda hadi leo nimepokea fedha ndiyo naamini, hata wazazi wangu hawajui hili swala nimeamua kuja mwenyewe kama mtoto wa kiume na nashukuru kweli nimeshinda,” ameeleza. Kwa ligi ya England, Meshack anashabikia timu ya Manchester United, Hispania anashabikia Barcelona, Ujerumani anashabikia Bayern Munich na Italia anaishabikia Juventus.  
4
Katika promosheni hiyo iliyoanza mwishoni mwa Novemba mwaka jana, inayolenga kurudisha sehemu ya pato la kampuni kwa jamii inayoizunguka, wateja 82 wameibuka washindi katika droo za kila siku na kila wiki.Akizungumza baada ya kupata washindi wa wiki ya kwanza ya awamu ya pili ya promosheni , katika droo iliyochezwa juzi, Meneja wa Huduma za Kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayuni alisema zaidi ya Sh milioni 324 zilitengwa kama zawadi ya fedha taslimu kwa ajili ya promosheni.“Mwenendo wa washiriki wa Mimi ni Bingwa kuendelea kujikusanyia pointi unazidi kuvutia. Watu wengi wameona kuwa wakicheza zaidi, wanajikusanyia pointi zaidi na hivyo kujiongezea nafasi zao za ushindi katika promosheni.Bado kuna zawadi nyingi zaidi kushindaniwa, ikiwemo zawadi kubwa ya Shilingi milioni 50,” alisema Hawa.Mmoja wa washindi wa droo ya wiki hii, Saidi Abdallah Kitambuliyo, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kiwalani, Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam, aliishukuru Kampuni ya Airtel kwa kumsaidia kuanza mwaka mpya wa 2014 kwa kishindo.Alisema fedha hizo amejishindia wakati muafaka ambapo bajeti yake kwa Januari 2014 ilikuwa imekausha akiba zake zote. Ninafuraha kubwa kuwa nitauanza mwaka 2014 kwa kishindo,” alisema.Bayuni alisema washindi wa tiketi watapata fursa ya kuchagua mtu mmoja wa chaguo lake atakayeongozana naye kufurahia safari iliyolipiwa gharama zote za kwenda kuangalia mechi moja kwa moja ) za klabu ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford, Uingereza.
5
Tanzania Prisons inatarajia kupambana na Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine.Mpalile alisema hasira za kufungwa na Yanga wanakwenda kuzimalizia kwa Mbeya City japo wanafahamu ni timu nzuri na inafundishwa na mwalimu mzuri.“Tumefungwa na Azam FC mabao 2-1 tukafungwa na Yanga mabao 3-0, ni matokeo mabaya kwetu, hivyo hasira zetu tutazimalizia kwa Mbeya City japo tunapokutana nao mchezo huwa mgumu,” alisema Mpalile.Pia Mpalile alisema dakika 20 za mwanzo walicheza kwa kuzuia zaidi huku wakitumia nguvu kutokana na maelekezo ya kocha kuona Yanga wanafanya mashambulizi yao kupitia wapi na kusahau kwenda kushambulia.Mpalile alimtupia lawama golikipa wao na kusema mabao mawili ya mwanzo walifungwa kutokana na makosa yake, lakini wanamheshimu kwa sababu ni makosa ya mchezo ambayo hata mchezaji mwingine anaweza kufanya.Pia nahodha huyo amekiri kadi nyekundu aliyooneshwa beki wao Josephat ilikuwa sahihi kwa sababu alikuwa ni mchezaji wa mwisho alipomfanyia Msuva rafu ya nyuma ‘tackling from behind’ akiwa ndani ya eneo la hatari.Mpalile pia alisema kubadilisha makocha kwenye timu inachangia timu yao kufanya vibaya kwasababu kila kocha anakuja na falsafa yake, hivyo inakuwa vigumu kubadilika haraka kuendana na matakwa ya kocha.
4
['Arsenal inataka kumsaini winga wa Barcelona Malcom, 22, huku Everton ikiwa tayari imewasilisha ofa ya dau la £31.5m kumsaini raia huyo wa Brazil. (Sun)', 'Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Dean Saunders anaamini kwamba Ole Gunnar Solskjaer hatomaliza msimu huu kama mkufunzi wa Manchester United . (talkSPORT) ', 'Solskjaer ana matumaini atafanikiwa kumnunua beki wa leicester Harry Magwire mbele ya majirani za wao wakuu Manchester City. (Mail)', 'Kiungo wa kati wa Manchester United na Uhispania Juan Mata, 31, amekataa mshahara wa £550,000 kwa wiki kutoka kwa klabu ya Shanghai SIPG na akaamua kuandikisha kandarasi mpya na klabu hiyo ya Old Trafford. (90Min)', 'Mata anasema kuwa alitia saini kadarasi mpya kwa kuwa klabu hiyo ni miongoni ma klabu kubwa nne duniani. (MUTV)', 'Ofa ya Everton ya dau la Yuro 30m limekataliwa na Juventus kumnunua mshambuliaji wa Itali Moise Kean. (Tuttosport, via Sport Witness)', 'Newcastle United ilimpatia mkufunzi Sam Allardyce ofa ya kurudi na kuifunza klabu hiyo wiki iliopita , lakini alikataa fursa hiyo.. (Mail)', 'Roma Ina hamu ya kumsajili beki wa Tottenham Toby Alderweireld na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 ana kifungu cha kumuachilia chenye thamani ya £25m . (Sky Sports)', 'Everton imewasilisha ombi la kumsaini mshambuliaji wa Lille Nicolas Pepe. Mchezaji huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 24 ataigharimu the tofees dau litakalovunja rekodi la £58.5m. (Telegraph)', 'Kiungo wa kati wa Southampton ,25 Mario Lemina, ambaye anatakiwa na Man United Arsenal na Leicester, amesema kuwa hataki kuichezea klabu hiyo msimu ujao.. (France Football, via Daily Echo)', 'Tottenham wanaimarisha ombi lao la kutaka kumsaini kiungo wakati wa Real Madrid Dani Ceballos, 22, kwa mkopo. (Mirror)', 'Arsenal inajiandaa kuongeza mabeki Calum Chambers, 24, Carl Jenkinson, 27, ama kiungo wa kati Mohamed Elneny, 26, katika makubaliano ya kumsaini winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha. Ombi la The Gunners la £40m kumnunua mchezaji huyo 26 limekataliwa . (Mirror)', 'Manchester City iko tayari kumzuia kiungo wa kati Fabian Delph msimu huu licha ya uvumi unaomuhusisha mchezaji huyo mwernye umri wa miaka 29 na uhamisho wa kuondoka Etihad. (Metro)', 'David Luiz anaamini kwamba kurudi kwa Frank Lampard katika klabu ya Chelsea utaifanya klabu hiyo kutambua umahiri wake.. (Standard)']
4
UTAFITI uliofanywa na Taasisi ya Twaweza, umebaini zaidi ya nusu ya Watanzania hawajisikii huru kumkosoa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu. Katika utafiti huo ambao unawakilisha Tanzania Bara peke yake, nusu ya wananchi ambao ni sawa na asilimia 47, hawajisikii huru kuwakosoa mawaziri na asilimia 46, wakuu wa mikoa na asilimia 43, wakuu wa wilaya. Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, wakati anatoa matokeo ya Twaweza yaliyotokana na utafiti huo. Eyakuze alisema takwimu za muhtasari huo wa utafiti zinatokana na utafiti wa Sauti za Wananchi ambao huratibiwa na taasisi yao. Alisema Sauti za Wananchi ni utafiti wenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za mikononi. Eyakuze alisema wananchi wanaendelea kuunga mkono kwa kiwango kikubwa upatikanaji wa taarifa. “Wananchi 7 kati ya 10 wanasema taarifa zinazomilikiwa na mamlaka za umma ni mali ya umma, ni asilimia 70 juu zaidi kutoka asilimia 60 mwaka 2015. “Na wananchi 9 kati ya 10 wanasema wananchi wa kawaida wapate taarifa zinazomilikiwa na mamlaka za umma kwa asilimia 86 juu zaidi kutoka asilimia 77 mwaka 2015 na kwa kuwapa wananchi uwezo wa kupata taarifa kunaweza kupunguza rushwa asilimia 86, juu zaidi kutoka asilimia 80 mwaka 2015. “Pamoja na kuunga mkono kwa kiwango kikubwa upatikanaji wa taarifa, wananchi 9 kati ya 10 hawajawahi kuomba taarifa kutoka katika ofisi za Serikali kwa asilimia 95, mamlaka za maji asilimia 93 , au vituo vya afya asilimia 93,” alisema. Alisema utafiti unaonyesha wananchi wameendelea kutumia vyanzo vile vile vya habari bila kuwa na mabadiliko makubwa isipokuwa kwa upande wa runinga. Eyakuze alisema mwaka 2013 runinga ilikuwa ni chanzo kikuu cha taarifa kwa asilimia 7 ya wananchi na mwaka 2017 ni asilimia 23 ya wananchi. Hata hivyo, alisema imani kwa aina mbalimbali za vyanzo vya habari inashuka; radio kutoka asilimia 80 mwaka 2016 hadi asilimia 64 mwaka 2017, runinga kutoka asilimia 73 mwaka 2016 hadi asilimia 69 mwaka 2017 na maneno ya kuambiwa kutoka asilimia 27 mwaka 2016 hadi asilimia 13 mwaka 2017. “Idadi kubwa ya wananchi pia wanasema Serikali ipate ridhaa ya mahakama katika kufanya maamuzi yoyote ya kuliadhibu gazeti kwa kutoa taarifa zenye maudhui yasiyofaa kwa asilimia 54. “Japokuwa wananchi wana mtazamo thabiti kuhusu upatikanaji wa taarifa na uhuru wa kuzungumza, ni wananchi wachache sana wanaofahamu sheria zinazohusiana na masuala ya habari,” alisema. Kuhusu sheria inayofahamika zaidi katika suala hilo ni Sheria ya Makosa ya Mtandao (2015), ambayo inafahamika na asilimia 10 ya wananchi huku asilimia 4 pekee ya wananchi wakifahamu Sheria ya Huduma za Habari (2016). Akifafanua kuhusu utafiti huo, alisema ni uwakilishi wa Tanzania Bara pekee, Zanzibar haihusiki. Takwimu za muhtasari huo zilikusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,519 kutoka awamu ya 25 ya kundi la pili la Sauti za Wananchi, na zilikusanywa kati ya Novemba 7 na Novemba 27 mwaka 2017.
3
JOSEPH HIZA NA MTNDAO PAMOJA na sifa ya utajiri wa kiuchumi na rasilimali likichukuliwa kama Taifa lililostawi zaidi kimaendeleo barani Afrika, wengi hufikiria mara mbili mbili kuitembelea Afrika Kusini kitalii, kimasomo au kikazi. Kundi hilo halihusishi wale vijana wanaozamia nchini humo kwa njia haramu kutafuta maisha wakiishi kigheto gheto na kuchanganyika na wenyeji, ambao hata hivyo mara nyingi huwapokea vibaya kwa mtazamo finyu kwamba ndio wachawi wa maendeleo na ustawi wao binafsi nchini mwao humo. Hata hivyo, si wahamiaji haramu tu wanaopokewa vibaya na wenyeji bali pia wale waingiao kihalali hasa wenye ngozi nyeusi, huhesabiwa wamo humo kuwapora ajira, ambazo wao wenyewe mara nyingi huzisusa kwa sababu mbalimbali. Sababu hizo ni kama vile uvivu, rekodi zao chafu kazini, kuchagua kazi, au mmiliki wa kampuni kwa vile wapo kwa sababu za kihistoria hawataki kufanya kazi kwa wazungu wa humo. Ukiachana na ubaguzi huo wa wenyeji, ambao si makusudio ya makala haya, kuogopwa kwa Taifa hili na wageni kunatokana na kufahamika kwake kama moja mataifa vinara duniani kwa kiwango kikubwa cha uhalifu. Uhalifu huo ni pamoja na mauaji, mashambulizi, uvunjaji majumba, ubakaji na machafuko mengine ya kihalifu. Kwa maneno mengine, Afrika Kusini inaongoza barani Afrika kwa vitendo vya mauaji yanayotokana na uhalifu. Ndiyo maana vitongoji vingi ndani ya taifa hilo katika majimbo na miji mbalimbali ikiwamo Johannesburg, Capetown vina vibao vinavyotahadharisha watu kuwa wanakaribia au wako eneo hatari kwa ubakaji, uuaji, utekaji nyara, uporaji na kadhalika. Hali na vitendo hivyo, wakati vikiijengea Afrika Kusini taswira mbaya vimechangia kukwamisha ukuaji wa uchumi wa taifa hilo kutokana na watalii kuogopa au kuikimbia kabla hawajamaliza ziara zao baada ya kukumbana au kunusurika na uhalifu. Mbali ya utalii, uwekezaji wa kigeni unadorora kutokana na hofu kuwa uhalifu unatishia maisha yao au uwekezaji wao huo. Kwa mujibu wa takwimu zilizosomwa na Waziri wa Polisi, Bheki Cele hivi karibuni, kwa wastani kuna matukio 57 ya mauaji kwa siku. Kiwango hicho cha mauaji nchini Afrika Kusini, ambacho tayari kiko juu kwa viwango vya dunia, kimeongezeka kwa asilimia saba, na kumlazimu waziri huyu anayehusika na jeshi la polisi kuilinganisha hali hiyo na ‘uwanja wa kivita. Jeshi la Polisi lilitoa takwimu za uhalifu Jumanne wiki hii zikionyesha kuwa watu 20,336 waliuawa nchini Afrika Kusini kati ya Aprili 2017 na Machi 2018, ikilinganishwa na watu 19,016 waliouawa katika kipindi kama hicho mwaka uliotangulia (Yaani Aprili 2016-Machi 2017). Cele anasema kiwango hicho cha juu cha mauaji “kinakaribiana na uwanja wa kivita – wakati kuna amani na hakuna vita. Matukio mengi ya mauaji yamehusishwa na vurugu za magenge ya uhalifu katika mkoa wa Cape Magharibi, ambao mji wake mkuu ni Cape Town. Kamati ya Bunge inasema juhudi za polisi kukabiliana na tatizo hilo hazijakuwa na ufanisi na kwamba makamanda wanapaswa kuimarisha uwepo wa usimamizi wa sheria katika maeneo yenye matukio mengi ya uhalifu. “Kamwe isitokee tena tukaja hapa kutoa takwimu kama hizo. Haiwezekani Waafrika Kusini wanaishi katika hofu kama hiyo, msongo kama huo na mauaji kama hayo,” anasema Cele. Matukio ya mauaji yaliongezeka kwa asilimia 6.9 katika mwaka wa kifedha wa 2017-18, ikilinganishwa na kipindi kilichotangulia, kwa mujibu wa takwimu hizo. Mauaji ya wanawake na watoto yaliongezeka pia. Ubakaji uliongezeka kwa asilimia 0.5, ambapo matukio 40.035 yalirekodiwa ikilinganishwa na matukio 39,828 ya mwaka uliotangulia, kwa mujibu wa takwimu hizo za polisi. Ingawa Afrika Kusini inajulikana kimataifa kwa uhalifu wake wa vurugu, lakini takwimu za kila mwaka zimekuwa zikipingwa mara kwa mara, hususani kuhusu ubakaji. Ongezeko kwa ujumla ni ongezeko la mara moja kubwa kabisa tangu kumalizika kwa utawala wa kibaguzi wa makaburu miaka 24 iliyopita, wachambuzi wa mambo wanasema. Takwimu hizo zinafifisha juhudi za Rais Cyril Ramaphosa, ambaye aliingia madarakani Februari mwaka huu akiahidi kuvutia uwekezaji wa kigeni nchini Afrika Kusini na kuchochea sekta ya utalii ya nchi hiyo. Takwimu zinaonesha ongezeko kubwa la mashambulizi ya kingono kufikia 50,108 kutoka 49,660 mwaka 2016-17. Makosa mengi ya kingono yaliyorekodiwa yalikuwa ya ubakaji. Hata hivyo, kuna ongezeko la idadi ya majambazi wanaovunja makazi ya watu, wanaokwapua mitaani na uchomaji moto watu au makazi. Kwa wastani kiwango cha uhalifu kilikuwa chini kwa zaidi ya asilimia nne. Cele, ambaye amekuwa Kmishina wa Taifa wa Polisi tangu Oktoba 2011 wakati aliposimamishwa  kwa tuhuma za ufisadi, alisema Waafrika Kusini wanapokuwa barabarani wanalazimika kuwa waangalifu vinginevyo watatekwa au wawapo nyumbani wanatakiwa kujilinda mapema kwani nyumba au milango huweza kuvunjwa ghafla na kuanza kutembeza unyama kwa familia. Gareth Newham, mtaalamu wa masuala ya uhalifu katika Chuo cha Masuala ya Usalama mjini Pretoria, alisema kiwango cha mauaji kinatambulika kama kiashiria cha machafuko Afrika Kusini”. Wataalamu wa masuala ya usalama wanasema kuna ongezeko la kiwango cha mauaji kipindi cha miaka mitano iliyopita baada ya kuanguka kwa asilimia 55 kipindi cha miaka 17. Ongezeko hilo wanasema linatokana na sababu mbalimbali ikiwamo kukithiri rushwa katika jeshi la polisi, nyadhifa za juu katika vyombo vya uzingatiaji sheria kuteuliwa kwa kuzingatia uaminifu na viongozi wanasiasa badala ya sifa stahili. Lingine walisema ni kuzorota kwa mazingira ya uchumi hali inayosababisha pamoja na mambo mengine ukosefu wa familia, ambao unaenda kuigusa familia au kaya nzima. Takwimu hizo zinakuja wiki moja baada ya takwimu nyingine rasmi z uchumi kuwashngaza wengi baada ya kufichua kwamba nchi ilikuwa katika mdororo wa uchumi. Sarafu ilianguka kwa kiwango cha chini, ambacho hakikuwahi kuonekana tangu Ramaphosa aingie madarakani. Wabashiri wa uchumi wanasema ukuaji wa uchumi mwaka huu kuwa chini ya asilimia moja mwaka huu. Tatizo la ukosefu wa ajira tayari liko juu linazidi kukua na mfumuko wa bei kuumiza bajeti za watu masikini vibaya sana. Hali ya ukosefu wa usawa na sababu nyingine kuu inayochochea uhalifu wa aina zote nchini Afrika Kusini, tafiti zilizopita zimethibitisha. Kwa msingi huo taifa hilo kamwe halitapunguza kiwango cha uhalifu wa aina zote iwapo uchumi hautakua na pengo la ukosefu wa usawa kupunguzwa. Sababu hizo ikiwamo zinazochangiwa na sababu ya kihistoria ambayo weusi walinyanyaswa na weupe walioshikiliwa uchumi zinalifanya Taifa hilo kuwa tofauti na mengine. Katika mataifa mengine kuna na yenye hali mbaya mno kiuchumi lakini hazina kiwango cha mauaji yanayotokana na uhalifu cha kutisha kama hicho cha Afrik Kusini.
0
 Na RAMADHAN HASSAN–DODOMA  ZAIDI ya abiria 150 wamenusurika kifo huku 32 wakijeruhiwa baada ya gari aina ya Isuzu kuigonga treni iliyokuwa ikitokea Kigoma kuelekea Jijini Dar es salaam katika eneo la Hazina jijini hapa.  Akizungumza na Waandishi wa Habari, jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, alisema treni hiyo  ilikuwa na mabehewa 14 ambapo mawili yalianguka na kusababisha ajali hiyo. Alisema ajali hiyo imehusisha gari lenye namba za usajili T 860 APW aina ya Isuzu huku akitaja chanzo cha ajali hiyo kuwa ni uzembe wa dereva wa gari kutochukua tahadhari alipokuwa akivuka makutano ya reli. Alisema mara baada ya gari hilo kuzima, dereva wake Hamisi Salum (49), Mkazi wa Nkuhungu jijini Dodoma, aliruka na kukimbilia na baadaye kujisalimisha polisi. Alisema treni hiyo ilikuwa ikitokea Kigoma  kupitia Mwanza na Mpanda kuelekea Dar es salaam ikiwa na behewa tisa za daraja la  tatu, mbili daraja la kwanza, mgahawa mmoja, behewa la vifurushi na behewa la breki.  “Majeruhi 10  wamelazwa katika hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma wodi namba 1,16 na 17, wengine tumewaruhusu waendelee na safari,”alisema  Kamanda Muroto Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Dk. Abul Pumzi, alisema majeruhi wa ajali hiyo wanaendelea kupata matibabu katika Hospitali hiyo.
3
RAIS Uhuru Kenyatta ameonesha kuguswa na kero ya maelfu ya wakulima wa mahindi ambao wamecheleweshewa malipo ya mazao yao.Akizungumza kwenye Maonesho ya Kilimo ya Nairobi, Rais Kenyatta alisema serikali iliwatengea wakulima pesa kwenye bajeti ya mwaka uliopita, lakini maofisa wa Bodi ya Nafaka (NC PB) wakaamua kuwalipa wafanyabiashara badala ya wakulima.“Lazima ukweli usemwe. Pesa za kulipa wakulima wa mahindi zilikuwa kwenye bajeti ya mwaka uliopita. Watu wa NC PB badala ya kulipa wakulima halisi walianza kulipa matajiri wafanyabiashara na kumalizia pesa, badala ya kulipa mkulima yule aliyetoa jasho,”alisema. Rais Kenyatta aliwaambia maofisa wa bodi hiyo kutorudia kitendo hicho, vinginevyo atawachukulia hatua kali za kinidhamu.“Nawahakikishia na ninaapa mbele ya Mungu, jaribuni hivyo tena na mtaona kitakachowatendea. Sisi hatutaki mchezo tena kwa sababu tumeona yale ambayo mmefanya na wale ambao walifanya tutawafuata.Pesa ya serikali ni ya mwananchi, kwanza lipa mwananchi yule ambaye ametoa jasho ya kulima shamba lake,”alisema. Wakulima hao walianza kulipwa Alhamisi, japo baada ya kulalamika mara nyingi na hata viongozi hasa wa kutoka North Rift kutishia kuongoza maandamano ya kushinikiza wakulima kulipwa.Rais Kenyatta alisema kilimo cha mahindi kimezidi kushamiri, akisema mavuno ya zao hilo mwaka huu yamepanda hadi magunia milioni 41, ikilinganishwa na magunia milioni 34 msimu uliopita, huku mavuno mengine zaidi yakitarajiwa.Aliongeza kuwa ikizingatiwa kuwa hadi sasa bado kuna magunia milioni 9.8 kwenye hifadhi, hiyo itamaanisha kuwa mwaka huu kutakuwa na magunia milioni 56 ambacho ni kiwango cha juu ikilinganishwa na kiwango linalotumia taifa kila mwaka cha magunia milioni 52.
3
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema mwaka 2015/16 serikali imefanya utafiti na kubaini katika kila watoto wa kike 100, watoto 27 nchini wanakuwa wamepata watoto kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.Ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa siku mbili uliowakutanisha wadau wa elimu kupinga mimba za utotoni ulioandaliwa na Taasisi ya Girls Inspire ya nchini Canada kwa kushirikiana na Australia.Alisema pia watoto wa kike wawili kati ya watano wanaolewa mapema kabla ya kufikisha miaka 18 wengi wao wakiolewa na wanaume waliowazidi umri.alisema madhara ya ndoa na mimba za utotoni nchini ni makubwa kwani licha ya mtoto wa kike kupata matatizo ya kiafya akiwa mdogo, pia husababisha kukosa elimu na hatimaye kuwa masikini kwa kushindwa kutimiza ndoto walizojiwekea.“Kama serikali tumeshachukua hatua kuwaokoa watoto wa kike na mimba na ndoa za utotoni. Uamuzi wa Rais John Magufuli kuanzisha sera ya elimu bure umeongeza fursa za watoto wa kike na kiume kupata elimu za msingi na sekondari…pia ujenzi wa mabweni 530 katika shule za sekondari umechangia kupunguza tatizo la mimba na ndoa za utotoni. Pia serikali imejenga vyoo zaidi ya 6000 na kurekebisha sheria. Mtu akioa mtoto atakuwa ametenda kosa la jinai na adhabu ni kifungo miaka 30 jela,” alisema.Alisema mwaka 2016 serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya jinsia walifanya utafiti uliobaini kuwa umasikini ndio chanzo cha uwepo wa ndoa na mimba za utotoni nchini.“Wazazi wengi huruhusu watoto wao kuolewa na kupata mimba za utotoni kwa sababu watapata mahari ambayo ni ng’ombe, fedha, pombe, asali, karanga na hii yote inatokana na suala la umasikini uliokithiri. Lakini pia zipo mila na desturi zinazomkandamiza mtoto wa kike kwamba nafasi yake ni jikoni,” alisema.Aliwataka waagizaji na watengenezaji wa taulo za kike nchini kupunguza gharama za uuzaji wa taulo.“Nimeshamwandikia Waziri wa Viwanda na Biashara na Waziri wa Fedha na Mipango, kuwataka waingizaji na watengenezaji wa taulo hizo kushusha gharama. Bei haijapungua, inabidi tuirudishe maana haijaleta tija kwa watoto vijiji ambao hawana uwezo wa kununua taulo hizo kwa Sh 2000,” alisema.Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha alisema ndoa na mimba za utotoni zinamfanya mtoto wa kike ashindwe kusonga mbele hivyo serikali itaendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha watoto wa kike wanabaki shuleni na kutimiza ndoto zao.Alisema serikali imeendelea kujenga shule nyingi na kuondoa ada ili watoto wa kike wapate fursa ya kusoma na kufanikiwa kimaisha.
3
Na ASHA BANI -DAR ES SALAAM MWENYEKITI wa Mtandao  wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo, amesema anahitaji kupumzika kwa sababu hayupo vizuri kiakili. Akizungumza  jana baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam akitokea mkoani Iringa baada ya kupata dhamana juzi dhidi ya kesi inayomkabili mahakamani, Nondo alisema anahitaji kupumzika  lakini muda si mrefu atawaelezea Watanzania yaliyomkuta hadi alipopata dhamana. Alisema akiwa katika mapumziko atakuwa anaandaa waraka ambao unaweza kuwa tayari ndani ya siku mbili ambao utaelekeza kwa kina yaliyomsibu hadi kufikishwa mahakamani. “Kwa sasa ‘mentally’ (akili) siko vizuri lakini nikitulia nitaweza kuzungumza, ndani ya siku 20 zikiwemo tatu za kukaa mahabusu Iringa hadi kupata dhamana,’’ alisema Nondo. Alipoulizwa kuhusu kusimamishwa chuo na uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema hajui lolote na hata barua ya kusimamishwa hajakabidhiwa hadi sasa . Pamoja na mambo mengine, mwanafunzi huyo amewashukuru  Watanzania waliopasa sauti zao  hasa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu na Jeshi la Magereza mkoani Iringa alilokaa nalo vizuri. Kwa upande wa Mratibu wa THRDC, Onesmo ole Ngurumwa alisema watakwenda mahakamani kupinga aumuzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kumsimamisha masomo Nondo kwa ajili ya kesi inayomkabili ambayo kwa sasa ipo mahakamani. “Na ndiyo maana hata Mahakama ya Iringa ilisema kuwa  wampe dhamana kwa kuwa mwanafunzi ili aweze kuendelea na masomo lakini wao wanamsimamisha, atasoma lini? “Na kama ikija kubainika kwamba hakufanya kosa watafanyaje wakati wenzake walikuwa wakiendelea na masomo? huu ni uonevu ambao hautakiwi kuvumiliwa,’’ alisema Olengurumwa. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo-Bisimba, alisema kilichofanywa na UDSM ni uonevu ikizingatiwa mazingira magumu aliyonayo na kitendo cha kumuweka ndani kwa muda mrefu. “Hata kanuni zilizopo chuoni hapo hazifai kutumika kutokana na kwenda kinyume na sheria na haki za binadamu,” alisema. DARUSO Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), imeshangazwa na kitendo cha kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii barua ya kusimamishwa masomo kwa Abdul Nondo kabla hajakabidhiwa mwenyewe. Rais wa Daruso, Jeremiah Jilili ameikosoa barua hiyo kuwa ina makosa mengi na ikiwamo kukosewa kwa kozi anayosoma Nondo Mwisho.   Biteko aeleza madini ujenzi yanavyoingiza fedha Na VERONICA SIMBA -DODOMA NAIBU Waziri wa Madini, Doto Biteko amesema madini ya ujenzi na viwanda yanaingizia Serikali kiasi kikubwa cha fedha ikilinganishwa na aina nyingine za madini yanayopatikana nchini. Akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Madini Dodoma akiwa kwenye ziara ya kazi, Biteko alisema takwimu zinaonyesha mwaka 2016/17, tani milioni 15.6 za madini ya ujenzi zilizochimbwa, ziliingiza Sh. bilioni 230.6. “Kati ya fedha hizo, ulipatikana mrabaha wa Sh bilioni 7.1,” alisema Biteko. Alisema pia idadi ya wachimbaji wa dhahabu na madini mengine nchi nzima wakijumlishwa, hawawezi kufikia hata robo ya wale wanaofanya shughuli za madini ya ujenzi. Alisema Serikali imejipanga kuhakikisha inaongeza vituo vya madini ya ujenzi na viwanda kutoka 85 vilivyopo sasa nchi nzima hadi kufikia 174. “Nina uhakika tukiviongeza vituo kufikia idadi hiyo, tutakusanya mrabaha wa zaidi ya Sh bilioni 15 katika madini hayo pekee,” alisema Biteko. Biteko pia aliwataka wakandarasi wanaotekeleza miradi mbalimbali hususani ya ujenzi wa barabara, watimize wajibu wao kwa kuzingatia sheria ya madini inayomtaka kila mtu aliyepewa leseni kulipa tozo na kodi stahiki. “Kama tuna Watanzania ambao ni maskini na tunachukua mrabaha kwao, halafu kampuni kubwa yenye mtaji mkubwa inayoendesha shughuli za ujenzi iache kulipa kodi stahiki, hiyo haikubaliki,” alisema. Biteko alisema, Wizara ya Madini itaandaa utaratibu wa kukutana na kujadiliana na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), ambao ndiyo hupewa leseni kwa mujibu wa sheria kuhusu namna bora ya kusimamia suala husika ili madeni yaliyopo yalipwe. Maagizo hayo ya Naibu Waziri Biteko yalikuja baada ya Ofisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma, Silimu Mtigile kumsomea ripoti iliyoeleza kuwa ofisi yake inakabiliwa na changamoto ya ukusanyaji mirabaha inayotokana na wakandarasi wa barabara. “Katika miradi mikubwa ya barabara iliyopo Dodoma, ulipwaji wa mirabaha ya madini ujenzi kutoka kwa wakandarasi umekuwa wa kusuasua ambapo hadi sasa kiasi cha Sh 642,632,195.00 kimekusanywa, sawa na asilimia 33.11 kati ya jumla ya Sh 1,941,177,853.23 zinazopaswa kulipwa,” alisema Mtigile. Mwisho.   Mwasisi Chadema kuzikwa Dar kesho Na TUNU NASSOR -DAR ES SALAAM MWILI wa aliyekuwa Katibu Mtendaji na Mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Victor Kimesera unatarajiwa kuzikwa kesho mchana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Akizungumza jana na MTANZANIA, msemaji wa familia, Mali Kimesera alisema ibada ya mazishi itaanza saa nne asubuhi nyumbani kwa marehemu, Mtaa wa Uporoto, Victoria Mwananyamara jijini hapa. Alisema kwa sababu kesho ni Alhamisi Kuu, mazishi yatafanyika saa saba mchana ili kutoa fursa kwa watakaokwenda katika ibada za siku hiyo. “Tunatarajia kuanzia ibada ya mazishi saa nne asubuhi ili kutoa nafasi kwa wataokwenda katika ibada ya Alhamisi Kuu,” alisema Mali. Kimesera alifariki Machi 24, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), alipokuwa akipatiwa matibabu.
3
NYOTA wa mpira wa kikapu duniani, Mmarekani Kobe Bryant na binti yake, Gianna, ni miongoni mwa watu tisa waliokufa katika ajali ya helikopta iliyotokea mjini Calabasas, California, Marekani, imeelezwa.Bryant aliyetamba katika mchezo huo, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 41, alikuwa akisafiri na helikopta yake binafsi, ambayo ilianguka na kuwaka moto na kuua watu wote waliokuwa ndani yake.Mkuu wa polisi wa LA alisema kuwa hakuna mtu aliyenusurika katika ajali hiyo iliyotokea baada ya helikopta hiyo kudaiwa kugonga mlima kutokana na ukungu uliomfanya rubani kushindwa kuona vizuri.Awali, ilielezwa kuwa helikopta hiyo ilikuwa na watu watano, lakini Polisi imethibitisha kuwa kulikuwa na watu tisa ndani yake na uchunguzi tayari umeanza ili kujua chanzo cha ajali hiyo, ambayo imempoteza gwiji wa mpira wa kikapu duniani.Bryant, ambaye ni bingwa mara tano wa Michuano ya Mpira wa Kikapu Ligi Kuu ya Marekani (NBA) mara tano alikuwa anatambuliwa duniani katika historia ya kuwa mmoja wa wachezaji bora wa vikapu.Salamu za rambirambi kutoka kwa watu maarufu na wachezaji wenzake nyota huyo zimekuwa zikimiminika zikionesha mshtuko wa kifo cha nyota huyo wa mpira wa kikapu.Viwanja vyote vya mpira wa kikapu nchini jana vilitenga muda wa kukaa kimya ili kutoa heshima kwa nyota huyo, ambaye aliichezea Lakers kwa misimu 20. Bryant atakumbukwa katika tuzo za Grammy (Gat the Grammy Awards), ambazo zilikuwa zikitolewa katika Uwanja wa Los Angeles Lakers, eneo ambalo alikuwa akichezea kipindi chote. “Tumechanganyikiwa na tuna uzuni sana kwa sasa,” alisema mtangazaji wa Grammys,Alicia Keys. “Kwa sababu mapema leo katika mji wa Los Angeles, Marekani na duniani kwa ujumla tumepoteza shujaa wetu mkubwa katika mpira wa kikapu, Kobe Bryant, ndio maana leo tumesimama katika nyumba aliyoijenga.”NBA katika taarifa yake ilisema kuwa imesikitishwa na ajali iliyosababisha kutoweka kwa uhai wa mchezaji huyo na binti yake, Gianna, mwenye umri wa miaka 13.“Kwa misimu 20, Kobe alituonesha kile ambacho kinawezekana kwa mtu ambaye ana kipaji na nia ya ushindi,” ilisema taarifa hiyo.AJALI ILITOKEAJE?Ofisa wa Polisi, Alex Villanueva alisema kuwa helikopta inaonesha kuwa ilikuwa na watu tisa wakati inaanguka, na kufuta tamko la awali kuwa huenda ilikuwa na watu watano ndani yake.Katika taarifa iliyotolewa na mji wa Calabasas zilisema kuwa wamepokea taarifa hiyo kwa maskitiko makubwa sana.“Ndege hiyo ilianguka nje kidogo ya mji wa Las Virgenes asubuhi kwa saa za hapa. Hakuna aliyenusurika katika ajali hiyo,” aliongeza mtoa taarifa huyo.Gavin Masak, alikuwa anaishi karibu na eneo tukio hilo lilipotokea, alisema kuwa helikopta hiyo ilianguka na kulikuwa na mlio mkubwa na baadae moshi kuonekana katika eneo hilo.Shuhuda mwingine alisema kuwa alisikia injini ikiwa kama ina shida hata kabla helikopta haijafika chini. Polisi wa LA wameonesha picha za tukio la ajali hiyo zikionesha gari la zima moto na moshi ukifuka kutoka milimani.Bodi ya Taifa ya Usafiri imeitambua helikopta iliyoanguka kuwa ni Sikorsky S-76B na imesema kuwa itatuma kikosi chake kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.BRAYANT NI NANI?Bryant alicheza mpira wa kikapu kwa misimu 20-katika viwanja vya Los Angeles Lakers, pamoja na mafanikio mengine mara 18 alikuwa NBA All Star na anashikilia nafasi ya kwa ufungaji wa pointi nyingi katika kipindi chote.Alistaafu mwaka 2016. Pia alitwaa tuzo ya mfungaji bora wa NBA pamoja na bingwa mara mbili wa mashindano ya Olympiki. Aliwahi kupata pointi 81 dhidi ya wachezaji wa Toronto Raptors mwaka 2006, katika historia ya michezo ya NBA.TUZO YA OSCARBryant alishinda tuzo za Oscar kama mchezaji wa filamu fupi mwaka 2018 filamu hilo ilikuwa ‘Dear Basketball’, filamu ya dakika tano iliyoangazia barua moja ya michezo aliyoandika mwaka 2015.Bryant na mke wake, Vanessa, walijaliwa kupata watoto wanne, ambao mbali na Gianna aliyefariki katika ajali hyo, wengine ni pamoja na Natalia, Bianca na Capri.Pia washiriki wa tuzo za Oscar mwaka huu walisimama kimya kwa dakika chache katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Lakers kumkumbuka Bryant, ambaye amecheza katika timu hiyo kwa misimu 20.
4
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma katika mwaka wa fedha 2019/20, imepanga kukusanya Sh bilioni 72.97 kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato ya ndani.Akiwasilisha Ripoti ya Mapato ya Jiji kwenye Baraza la Ushauri la Mkoa (RCC), Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji, Godwin Kunambi alisema makusanyo hayo katika mwaka huu wa fedha yameongezeka kwa Sh bilioni 5.8 ukilinganisha makusanyo ya mwaka jana, ambayo yalikuwa Sh bilioni 67.15. Alisema katika mwaka 2018/19, viwanja vilivyopimwa au kukasimiwa kwa watu vilikuwa 20,000, ambavyo vililiingizia jiji Sh bililioni 59.089 sawa na asilimia 37 ya bajeti yote ya mapato ya mwaka huo ambayo ni Sh bilioni 159.46.Alisema katika mwaka 2019/20, utegemezi wa viwanja utapungua, kwani vinavyokadiriwa kupimwa 10,000 vinategemewa kuingiza mapato ya Sh bilioni 49 ambayo ni sawa na asilimia 27 ya bajeti yote ya mwaka huu ambayo ni Sh bilioni 161.87. Alisema kati ya mapato hayo katika bajeti ya mwaka huu, Jiji linatarajia kupata Sh bilioni 23.97 kutoka kwenye vyanzo vingine vya ndani licha ya viwanja. Kunambi alisema pamoja na jiji kuweka mkakati wa kupunguza utegemezi wa viwanja na hivyo kupunguza upimaji wa viwanja kwa asilimia tano, bado bajeti ya mapato ya ndani imeongezeka kwa asilimia 8.7.Katika mkakati huo wa kupunguza utegemezi wa viwanja mwaka huu, jiji linategemea kupata mapato mengine kutoka kwenye ushuru wa huduma ya Sh bilioni 1.0, usafi wa mazingira Sh bilioni 1.405 na leseni za biashara Sh bilioni 1.125. “Mapato mengine linayotegemea ni kutoka kitengo cha ufyatuaji matofali ya Sh bilioni 1.0 pamoja na maeneo ya uwekezaji Sh bilioni 9.9. Vyanzo hivyo vya maeneo ya uwekezaji vitaanza kuingiza mapato nusu ya pili ya mwaka wa fedha 2019/20,” alisema.Mbunge wa Kondoa Mjini, Edwin Sanda (CCM) alisema katika miradi ya uwekezaji, jiji linatakiwa kuonesha kila mradi utatumia fedha kiasi gani na kuingizia faida kiasi gani. Akifunga RCC, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge alipongeza mkakati wa jiji katika kujikita katika uwekezaji. Alisema ili kuleta mafanikio mazuri, lazima kusimamia vizuri.
3
MABINGWA watetezi wa Michuano ya Chalenji kwa Wanawake ya Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), Kilimanjaro Queens jana imetinga fainali baada ya kuifunga Uganda kwa bao 1-0 katika nusu fainali kwenye Uwanja wa Chamazi , Dar es Salaam.Ushindi huo sasa unawafanya mabingwa hao mara mbili mfululizi kukutana tena na Kenya katika fainali itakayofanyika kesho kwenye uwanja huo. Kenya wenyewe walitinga nusu fainali baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Burundi katika mchrezo uliofanyika mapema jana kwenye uwanja huohuo.Bao pekee katika mchezo huo lililoipeleka Kilimanjaro Queens katika fainali lilifungwa katika za lala salama na Asha Rashid au Mwalala. Mchezo wa kusaka mshindi watatu nao utafanyika mapema kesho kwa kuzikutanisha Burundi iliyofungwa na Kenya wakikabiliana na Uganda waliofungwa na Kili Queens. Kocha wa Kili Queens, Bajari Shime aliwapongeza wachezaji wake kwa ushindi huo na kusema kuwa watarekebisha makosa yaliyojitokeza katika mchezo huo na kufanya timu yao kukosi mabao mengi.Alisema wapinzani wao Uganda walicheza kwa kujihami na kujiangusha mara kwa mara na hivyo kufanya mchezo kupooza, akisisitiza kuwa hiyo ndio mbinu yao waliyokuja nayo jana, lakini alishukuru kwa ushindi wa timu yake. Kocha wa Uganda, Farida Bugega aligoma kabisa kuzungumza kuhusu mchezo huo na badala yake kila alipoulizwa alisema: “No komenti”.Aidha katika mchezo ulitangulia wa nusu fainali, Kenya iliibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Burundi kwenye uwanja huohuo wa Chamazi. Kenya waliandika bao la kwanza katika dakika ya 14 lililofungwa na Dorcus Nixon kwa kichwa akiunganisha wavuni mpira wa kona wakati Jentrix Shikangwa aliifungia Kenya bao la pili katika dakika ya 54 baada ya kuwatoka mabeki wa Burundi na kuujaza mpira wavuni.Mwanalima Jereko alifunga bao la tatu katika dakika ya 67 baada ya kupiga shuti kali lililomshinda kipa wa Burundi, Annedy Kundu na kujaa wavuni. Kenya walipata bao la nne kupitia kwa Corazone aquaino kwa shuti kali baada ya kupokea pasi kutoka kwa Jereko katika dakika ya 77,
3
BEIJING, CHINA RAIS Xi Jinping amesema muungano kati ya China na Taiwan hauepukiki na harakati za kisiwa hicho chenye mamlaka ya ndani kutaka uhuru wake ni ndoto ya mchana. Akizungumza wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 40 tangu kutolewa kwa tamko muhimu juu ya sera ya China kuhusu Taiwan kwenye ukumbi maarufu wa umma mjini hapa jana, Xi alionya kuwa ikibidi hawatasita kutumia nguvu kulinda muungano huo. “Tuko radhi kuweka upeo mpana kwa ajili ya muungano kwa njia ya amani, lakini kamwe hatutaruhusu aina yoyote ya harakati za kuwania uhuru wa Taiwan,” alisema Xi huku akishangiliwa na wajumbe ukumbini hapo. China na kisiwa cha Taiwan kilichoko umbali wa kilomita 160 kutoka bara, zilitengana wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1949 baada ya upande wa wapiganaji wa kizalendo ulioshindwa kuamua kuunda Serikali yake kisiwani humo. Xi amependekeza kufanyika mazungumzo ya pande mbili, ya kuweka mpangilio wa kuzileta pamoja sehemu hizo mbili kwa njia ya amani, akisema watu wa pande zote wanataka kuona zikiungana na kuwa China moja. Alisema muungano huo unaweza kuwa wa mtindo wa ‘nchi moja-mifumo miwili’ ambao utaheshimu muundo wa kijamii wa Taiwan na mtindo wa maisha wa watu wa kisiwa hicho, wenye kuhakikisha haki na uhuru wao wa kidini, umilikaji wa mali na haki nyinginezo. “Lakini watu wote wanapaswa kuelewa jaribio lolote la kutangaza uhuru wa Taiwan litaleta janga kubwa kwa watu wa Taiwan,” alionya Rais Jinping. Haijulikani madai ya kiongozi huyo kuwa watu wa pande zote mbili wana kiu ya kuungana tena imepokewa vipi kisiwani Taiwan. Ni juzi tu, Rais wa Taiwan, Tsia Ing-wen alitamka bayana, kuwa watu wa kisiwa hicho wanaazimia kuendeleza utawala na uhuru wao wa ndani. Ingawa kwa wakati huu China na Taiwan zina uhusiano mzuri kibiashara na kitamaduni, Taiwan inayojivunia mfumo wake wa kidemokrasia, haionyeshi shauku ya kujiunga na China iliyo chini ya utawala wa chama kimoja.
2
WAKATI mashindano ya 17 ya dunia ya riadha yaanza leo Doha, Qatar, Tanzania inatupa karata yake ya kwanza kwa mwanariadha wake wa kike, Failuna Abdi kukimbia mbio za marathon. Failuna ambaye muda wake bora binafsi ni saa 2:27:55, mbali na kusaka medali ya kwanza ya Tanzania kwa wanawake katika historia ya mashindano hayo, pia atakuwa akitaka kuwa Mtanzania wa tatu kupata medali katika mashindano hayo.Christopher Isegwe ndiye alikuwa mwanariadha wa kwanza wa Tanzania kupata medali baada ya kushika nafasi ya pili katika mashindano ya dunia yaliyofanyika Helsinki, Finland mwaka 2005 na kurudi na medali ya fedha, huku Alphonce Simbu akitwaa shaba 2017 jijini London. Failuna aliondoka nchini mapema ili kuwahi mbio hizo za marathon za wanawake, ambazo Tanzania inawakilishwa na mwanamke mmoja tu, huku wengine watatu wakiume wakitarajia kuondoka nchini Oktoba 2 na wanatarajia kukim- bia Oktoba 5. Wanariadha wa kiume ambao nao watashiriki mbio za marathon zitakazofanyika Oktoba 5, siku moja kabla ya ufungaji wa mashindano hayo ni pamoja na Simbu, Stephano Huche na Augustino Sulle, ambaye anashikilia rekodi ya taifa ya marathon aliyoiweka Toronto, Canada Oktoba 21, 2018. Awali, rekodi hiyo ya taifa ya marathon ilikuwa inashikiliwa kwa muda mrefu na Juma Ikangaa kabla Sulle hajaivunja na kuishikilia hadi sasa. Kwa mujibu wa mtandao wa IAAF, tayari Failuna jina lake liko katika orodha ya wanariadha watakaoanza mbio hizo leo (startlist) pamoja na wengine 68, amnazo zinatarajia kuanzia majira ya saa tano usiku ili kuk- abiliana na joto kali la Doha. Kocha wa timu hiyo, Andrew Pamga akizungumza kwa njia ya simu kutoka Arusha jana alisema timu yake ilikuwa na changamoto kibao wakati wa maandalizi, lakini wanaridha wake wameahidi kuipigania bendera ya taifa na kurudi na medali kutoka katika mashindano hayo.Panga alisema timu hiyo haikuwahi kukaa kambi ya pamoja kutokana na matatizo ya fedha, lakini wamejiandaa vizuri na wana uhakika wa kurejea na medali, licha ya ugumu wa mashindano hayo. Nahodha wa timu hiyo ya riadha ya taifa, Simbu amekiri maanfalizi yao kukabiliana na ukata na kama sio kuwasaidia tiketi na baadhi ya watu, basi pengine Tanzania isingeshiriki kabisa mashindano hayo ya dunia.Alisema wanariadha wanaowakilisha timu ya taifa kila mmoja akifanya maandalizi kivyake na hawakuwahi kuwa pamoja kwa muda wote mpaka walipokutana siku wanaagwa. Timu hiyo iliagwa Jumatano jijini Arusha.
4
Serikali imewaagiza makatibu Tawala wa mikoa nchini na maafisa utamaduni kuhakikisha wanasimamia mchakato wa upatikanaji wa vazi la Taifa ili ukamilike haraka. Aidha, amesema wizara imeweka mkakati maalum kwa kushirikana na maafisa utamaduni ili kupata vazi la Taifa. Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza alitoa maagizo hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Wingwi, Juma Kombo Hamad(CUF). Katika swali lake, Mbunge huyo alisema ni muda mrefu Serikali ilikuwa kwenye mchakato wa kupata vazi la Taifa. ”Je, serikali imefikia hatua gani ya mchato huo, ni lini watanzania wategemee kuwa na vazi la taifa,”alihoji. Akijibu swali hilo, Shonza alifafanua kuwa mchakato huo ulianza 2003/4 na kufufuliwa tena mwaka 2011 baada ya kuona mitindo iliyopatikana haikidhi haja ya kuwa vazi la taifa. Alisema mwaka 2011 kamati ya kukamilisha mchakato wa kupata vazi la taifa iliteuliwa ambapo upatikanaji wa vazi hilo ulipitia hatua kadhaa. Alitaja baadhi ya hatua hizo ambazo ni wizara kushirikiana na wabunifu wa wanamitindo kwa lengo la kushirikisha wadau wa fani hizo na kupata vazi litakalotambulisha taifa. Alieleza kuwa baada ya kamati kumaliza kazi yake ilikabidhi wizarani taarifa na mapendekezo kuwa vazi la taifa litokane na aina ya kitambaa na sio mshono. Aidha, aina ya vitambaa kwa vazi hilo ilipendekezwa. Alifafanua kuwa Serikali kupitia Baraza la Mawaziri liliagiza kwamba jamii iachwe huru kuchagua aina ya vazi ambalo litatokana na mageuzi ya ndani ya jamii yenyewe na isiwe uamuzi wake. Shonza alieleza kuwa baadhi ya changamoto zilizojitokeza kwa kipindi hicho ni uhamasishaji hafifu wa uvaaji wa vazi la taifa na kwamba wananchi walitarajia kupokea vazi na sio kuoneshwa vitambaa.
1
KOCHA wa Lipuli FC, Suleiman Matola amesema kucheza kwa kujituma na kutanguliza malengo ni mbinu itakayokisaidia kikosi cha Simba kuibuka na ushindi kwenye mchezo wao kimataifa dhidi ya Nkana FC ya Zambia na kutinga hatua ya makundi.Mchezo huo wa raundi ya pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika, unatarajiwa kupigwa kesho kwenye uwanja wa taifa wa Dar es Salaam, baada ya ule wa awali uliopigwa Kitwe, Zambia wenyeji Nkana kupata ushindi wa mabao 2-1.Akizungumza na gazeti hili jana Matola, alisema bingwa huyo mtetezi wa Ligi Kuu ana kikosi kizuri na kipana na kwamba kinachotakiwa kwa wachezaji wake ni kufuata maelekezo ya kocha wao na kucheza kwa nidhamu ili kupata ushindi. “Wachezaji wa Simba wanatakiwa kujiandaa vizuri, wasibweteke na bao walilolipata ugenini, Nkana ni timu nzuri,hata wachezaji wa Simba ni wazuri pia kinachotakiwa kocha wa Simba Patrick Aussems kuhakikisha anatengeneza muunganiko mzuri wanaweza wakapata mabao mengi,”alisema Matola aliyewahi kuwa mchezaji wa kikosi hicho na hatimaye kocha msaidizi.Alisema wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanawazuia washambulia wa wapinzani wao wasipate nafasi ya kufunga bao na kuhakikisha wanatumia vyema nafasi watakazozipata ili kuhakikisha katika kipindi cha kwanza wanapata bao la mapema ili kuwachanganya wapinzani hao kama walivyofanya kwa Mbabane Swallows, eSwatini walioshinda jumla ya mabao 8-1.Katika mchezo huo wa kesho timu itakayoibuka na ushindi katika itafuzu hatua ya makundi. Ushindi wa bao 1-0 utaivusha Simba na kurudia historia ya mwaka 2003 ilipotinha hatua ya makundi kwa kuifunga Zamalek ya Misri. Nahodha wa timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 17, ‘Serengeti Boys’ Abraham Morice (kulia) akichezesha droo ya fainali za AFCON U-17 katika hafla iliyofanyika juzi Mlimani City, Dar es Salaam.Kushoto ni mchezaji wa zamani wa Taifa Stars, Adolf Rishard. (Picha na Rahel Pallangyo) JUVENTUS, Italia CRISTIANO Ronaldo anatarajiwa kucheza dhidi ya Roma leo kabla ya kupumzishwa katika moja ya mechi mbili za ‘fainali’ kwa mwaka 2018, Massimiliano Allegri alithibitisha. Bosi huyo wa Juve aliahidi nkumpa nyota huyo wa Ureno angalau mechi moja Desemba huku Ronaldo akicheza dakika 90 kwenye mechi zote za Serie A isipokuwa moja msimu huu.Allegri anataka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 kucheza dhidi ya Roma, wakati Juve ikiwania kuendeleza rekodi yake ya kutokufungwa katika kutetea taji lao, lakini anafuraha kuona Ronaldo akikosa safari ya kwenda Atalanta kwenye ‘Boxing Day’ au kwenye mechi dhidi ya Sampdoria Desemba 29. “Ronaldo atacheza kesho (leo), kisha atakosekana katika mechi mbili zijazo,” alisema Allegri kwneye mkutano na waandishi wa habari jana.Mechi ya leo katika uwanja wa Allianz Juve inakutana na Roma iliyocheza mechi tano mfululizo bila ushindi kwenye michuano yote kabla ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Genoa Jumapili iliyopita. Presha iko kubwa kwa kocha mkuu Eusebio Di Francesco, lakini Allegri alisisitiza ushindi. “Ni timu nzuri, pamoja na mambo mengine, ni timu pekee ya Italia pamoja na Juventus bado zipo kwenye Ligi ya Mabingwa,” alisema.
4
MBUNGE wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa ndoa yake na mumewe, Gustavus Babile haijawahi kuvunjika, kwani ndoa ya Kikristo huwa haivunjiki, ingawa hakuweka wazi kama wanaishi pamoja na mumewe huyo Mbweni, Dar es Salaam au la.Bulaya ambaye jana alikuwa akiendelea kutoa utetezi wake, kwa kujibu maswali ya upande wa mashtaka katika kesi ya uchochezi, inayowakabili viongozi wa Chadema, aliyasema hayo alipojibu maswali ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Simoni Wankyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.Alidai kuwa walifunga ndoa na Babile mwaka 2003 na ndoa yao haijavunjika. Akijibu swali la Mkurugenzi Msaidizi wa Mashtaka, Faraja Nchimbi kuhusu hati yake ya kusafiri, Bulaya alidai hakuna mahali hati hiyo imeonesha kugongwa mhuri wa kusafiri nje ya nchi kati ya Februari 16 hadi 28, 2018 na wala hajawahi kusema mahakamani, kama alisafiri nje ya nchi katika tarehe hizo.Alidai kuwa alichoieleza mahakama ni kuwa siku hiyo ya Februari 16, mwaka jana, aliwahi kuondoka katika mkutano wa kufunga kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Kinondoni, kwa kuwa mshitakiwa mwenzake, Halima Mdee ambaye ni jirani yake huko Mbweni jijini Dar es Salaam, alikuwa anaumwa hivyo walienda kujiandaa na safari ya kwenda kwenye matibabu Afrika Kusini.Kesi hiyo iliahirishwa hadi Januari 20 ambapo itaendelea kusikilizwa ushahidi kwa siku nne mfululizo hadi Januari 24, 2020. Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, Mbunge wa Kibamba ambaye sasa ni Katibu Mkuu, John Mnyika, aliyekuwa Katibu Mkuu, Dk Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu na wabunge Peter Msigwa (Iringa Mjini), John Heche (Tarime Vijijini), Esther Matiko (Tarime Mjini) na Halima Mdee (Kawe).Washitakiwa wanakabiliwa na mashitaka 13 likiwemo la kula njama, ambako wote wanadaiwa kuwa Februari 1 na 16, mwaka jana Dar es Salaam, walikuĺa njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali na kukiuka tamko kutawanyika.
3
Mwandishi Wetu,Dar es Salaam ZAIDI ya wafanyabiashara 2000 katika mkoa wa kodi wa Ilala wamepatiwa elimu ya kodi inayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini.Mamlaka hiyo imekuwa na ikifanya kampeni ya elimu ya kodi mara kwa mara kwa kuwafata wafanyabiashara kwenye biashara zao (mlango kwa mlango). Akizungumzai zoezi hilo Afisa Msimamizi wa Kodi wa mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Zakeo Kowelo alisema kuwa katika siku sita za zoezi hilo, jumla ya wafanyabiashara 2,165 wamepatiwa elimu mbalimbali ya kodi. Alisema maeneo ambayo wamewafikia wafanyabiashara na kuwapatia elimu ni Tabata, Relini, Bima, Liwiti, Barakuda, Kimanga, Segerea, Kinyerezi, Kisiwani na Bonyokwa Mkoa wa Kodi wa Ilala. Alisema zoezi limeenda vizuri na kwamba wafanyabiashara wametoa ushirikiano wa kutosha kwa kutoa taarifa muhimu na kuonyesha nyaraka ambazo zilihitajika jambo ambalo limewawezesha kuwapa ushauri na elimu inayostahili. “Kwa hili tunawashukuru sana kwani tumeweza kuwaelimisha kama tulivyopanga”, alisema KoweloAlisema zoezi lilihusisha kupita duka kwa duka na kuangalia taarifa za wafanyabiashara za kodi ambapo baada ya kuangalia taarifa walifanya majadiliano na kumshauri mfanyabiashara jinsi ya kutunza kumbukumbu. Aliongeza kuwa kwa wale ambao hawajasajili biashara zao wameelekezwa taratibu za kusajili ili watambulike kuwa walipakodi na kwamba pamoja na kusajili biashara pia wafanyabiashara wameshauriwa jinsi ya kujisajili na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na wale wanaostahili kutumia mashine za kodi za kielektroniki wamepewa utaratibu wa kupata na kuzitumia mashine hizo. “TRA ni sehemu ya biashara za wananchi hivyo lengo letu ni kuwaelimisha wananchi ili wafanye biashara kwa usalama zaidi na kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi sahihi na kwa wakati’, alisema Kowelo. Naye Stewart Kimbaga mfanyabiashara wa duka la urembo maeneo ya Bonyokwa alisema kuwa kampeni hiyo ya elimu ya kodi ni nzuri na kwamba itasaidia kutokana na kuwa baadhi ya wafanyabiashara hawana uelewa wa jinsi ya kufanya biashara ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kulipa kodi. Alisema hiyo ni fursa muhimu na kwamba ukaguzi peke yake hautoshi bali unatakiwa uambatane na elimu ili kuwaongezea wananchi uelewa na kujenga uhusiano mzuri baina ya TRA na walipakodi. Zoezi la kutembelea walipakodi katika maeneo yao ya biashara ni mkakati ambao TRA inautekeleza ili kuwaelimisha walipakodi, kuwapa ushauri wa kitaalamu kuhusu taratibu za kulipa kodi, kusajili biashara ambazo hazijasajiliwa, kuwakumbusha kulipa kodi, kutatua changamoto zinazo wakabili na kupata maoni yao kuhusu huduma inayotolewa na TRA kwa ajili ya kuboresha utendaji wake.
5
NA VERONICA ROMWALD-DAR ES SALAAM HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH), imesema  gharama inazotoza kulipia huduma ya kuhifadhi maiti haijapanda. Kauli hiyo imetolewa baada ya baadhi ya ndugu wa marehemu ambao hufikisha wagonjwa hao na kukutwa na  mauti hospitalini hapo, kulalamikia kupanda kwa gharama kimyakimya. Akizungumza na MTANZANIA mwishoni mwa wiki, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja Muhimbili, Aminiel Aligaesha,  alisema huwa wanatoza kiasi cha Sh 30,000 pekee kwa siku. “Majokofu yetu ni ya kiwango cha hali ya juu, yana uwezo wa kuhifadhi mwili wa marehemu hata mwaka mzima pasipo kuharibika. “Hii ni Hospitali ya Taifa, gharama hizi tunatoza kwa kipindi cha miaka sita sasa na hazijabadilika sijui watu kwa nini wanalalamika,” alisema. Alisema huwa wanatoza gharama hizo kwa ajili ya kuchangia ununuzi wa umeme. Alisema hata hivyo gharama hizo huweza kuongezeka iwapo ndugu wa marehemu watapenda kupatiwa huduma nyingine ikiwamo ile ya kusafisha maiti. “Sisi tunawajibika kuhifadhi mwili wa marehemu na kutoza fedha hizo kuchangia umeme na matengenezo kama yatahitajika kufanyika. “Lakini kama ndugu watapenda mwili uoshwe na au kurembwa basi hizo ni gharama nyingine ambazo watawajibika kuzilipa kulingana na huduma waliyopewa,” alisema.
3
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma iko katika mkakati kupata vyumba 52 vya madarasa kabla ya Februari 2, mwaka huu ili wanafunzi 2,610 waliofaulu na kukosa nafasi za kujiunga kidato cha kwanza wapate nafasi hiyo kusoma haraka.Akisoma ripoti mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge kabla ya kuanza ziara kukagua madarasa yatakapojengwa, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Hidaya Maenda amesema wamejipanga kumaliza upungufu huo."Ili kuhakikisha mpango huo unafanikiwa, Halmashauri imekaa na wakuu wa shule za sekondari zenye uhaba wa madarasa na kuweka mikakati kukamilisha miradi hiyo," amesema.Maeda alisema mkakati ni kujenga madarasa mapya 20 katika shule 11 zenye upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa. Alisema tayari ujenzi umeanza katika shule hizo.Amesema mkakati huo unalenga kukamilisha madarasa 40 kati ya madarasa 52 yanayotakiwa.Ofisa Elimu wa Sekondari wa Jiji la Dodoma, Abdallah Membe amesema lengo ni kuhakikisha ujenzi wa majengo unakamilika katika muda uliopangwa ili wanafunzi waanze kusoma.Alisema idara ya sekondari imeanza kutekeleza shughuli zake kulingana na miongozo na mpango wa kazi wa idara shule zote 56 zenye jumla ya wanafunzi 19,205 wapate elimu.Katika wanafunzi 10,103 waliofanya mitihani darasa la saba mwaka jana, wanafunzi 5,428 walipangwa kujiunga na kidato cha kwanza awamu ya kwanza na wanafunzi 2610 wanasuburi kukamilishja madarasa waende.Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Mahenge baada ya kufanya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa amepongeza Jiji kutenga sh milioni 20 kwa kila sekondari yenye upungufu wa madarasa akawataka viongozi kushirikiana kukamilisha majengo wanafunzi wasome.Alitawaka watendaji wa mitaa na vijiji kuwahimiza wazazi kuwapeleka watoto wote shuleni kutokana na idadi ndogo ya wanafunzi walioripoti 1,951 hadi Januari 9 mwaka huu.Aliwataka wazazi kutowaondoa shule watoto waliofaulu ili waende kufanya kazi za ndani au kuozesha, wakati halmashauri ya jiji inafanya jitihada kuhakikisha wanapata nafasi kusoma.
3
MAJADILIANO ya Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Tanga, yanaendelea huku serikali ikisema kasi yake ni kubwa, ambayo ikilinganishwa na nchi nyingine zilizowahi kufanya mchakato kama huo, haijawahi kuwa hivyo.Wakati mradi huo wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), unatarajiwa kutekelezwa Septemba mwaka huu, mchakato wa kulipa fidia watu watakaopisha ujenzi unaendelea, ikiwamo kutaarifu wananchi waliofanyiwa tathmini na kuwaonesha stahili zao kabla ya kuanza kulipa.Akizungumza na HabariLeo, Mratibu wa Mradi wa Bomba la Mafuta, Salum Mnuna alisema majadiliano hayo, yaliyoanza Julai mwaka jana yamefikia asilimia 80; na pande zote zimepeana malengo ya kukamilisha Septemba mwaka huu, hivyo kila nchi inafanyia kazi tarehe iwe imemaliza. “Tunakwenda vizuri kwa maana ya majadiliano. Katika mazingira ya duniani, speed (kasi) yetu ni nzuri hakuna waliowahi kufanya hivi… Nchi nyingine zote zinaenda hata miaka mitano,” alisema Mnuna. Aliongeza kwamba majadiliano hayo, yamechukua mwaka mmoja.Akisisitiza umakini wa serikali kuhakikisha haiingii kwenye mikataba mibovu, alisema yapo maslahi ya kibiashara, kisheria na sera ambayo misingi yake inapaswa isimamiwe na kukubaliana. “Kimsingi majadiliano yanaendelea, hatuwezi kwenda kutengeneza mikataba feki. Kwa hiyo mwezi wa tisa (Septemba) inatakiwa yakamilike ili kuweza kuwa na maamuzi ya mwisho ya kuanza ujenzi wa mradi,” alisema.Aliongeza kuwa serikali inaunga mkono yaende vizuri wafanye kwa usahihi. Kwa mujibu wa mratibu wa mradi, mkataba wa utekelezaji wa mradi baina ya nchi mbili na mwekezaji, ulitarajiwa kukamilika Juni mwaka huu ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema katika mkataba hodhi, Uganda ilikuwa nyuma na Tanzania ilikuwa mbele, ingawa inatakiwa wote wamalize pamoja, jambo lililosababisha mwekezaji kujielekeza zaidi na Uganda kuliko Tanzania.Alitaja mikataba mingine inayohusu mradi huo wa bomba la mafuta, inayotakiwa kujadiliwa ni wa ushirikiano wa ubia, bandari, kifedha na kiujenzi ambayo inategemea mkataba hodhi umalizike. “Mikataba mingine haina shida itaendelea. Mkubwa ni mkataba hodhi, ukishasainiwa mingine yote inakuwa mteremko,” alisema. Akizungumzia mchakato wa fidia, alisema kawaida wanafanya tathimini ambayo inapelekwa kwa Mthamini Mkuu kwa ajili ya kuziainisha.Baada ya hapo, zinapelekwa kwa wananchi wathibitishe na endapo yapo malalamiko, yanatatuliwa. Alisema, “Tuko hatua ya kuonesha wanaoguswa na mradi taarifa zao kwamba tumefanya hivi na stahili zao ni hizi na kisha wanasainishwa fomu. Tukimaliza, mthamini akaidhinisha, utaratibu wa malipo unaanza, fedha zinatolewa Hazina na kikosi kinaundwa,” alisema. Hivi karibuni, Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani akifungua Kongamano la Wadau wa Mkoa wa Kagera lililohusu mradi huo wa bomba la mafuta, alisema wananchi 10,000 watalipwa fidia kupisha mradi.Alisema katika mwaka huu wa fedha, zimetengwa zaidi ya Sh bilioni 50.7 kwa ajili ya fidia ya kupisha bomba hilo, lenye urefu wa kilometa 1,445. Alisema matarajio ni kuanza ujenzi Septemba mwaka huu, baada ya majadiliano baina ya pande zinazohusika na mradi huo kukamilika. Ikiwa ni sehemu ya hatua za utekelezaji wa mradi, Mei mwaka huu serikali ilizindua mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji, wilaya na mikoa itakayopitiwa na mradi. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alisema mpango huo wa matumizi ya ardhi, unahusisha mikoa minane, wilaya 24 na vijiji 226.
3
BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamiza wa Mazingira (NEMC) limekaribisha mradi wa utafiti wa kisomi, kabla ya uchimbaji wa urana (uranium) utakaohusisha Tanzania, Malawi, Namibia na Zambia.Akifungua jana mkutano wa siku moja wa wasomi na wadau wengine wa mazingira jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa NEMC, Dk Samuel Gwamaka, alisifu mradi huo kwa maelezo kwamba utafanya tafiti za kisomi, ambazo zitatoa mwelekeo thabiti wa kutunza mazingira ya Tanzania katika uchimbaji wa madini ya urana. "Huu ni mradi mzuri kwa sababu tafiti za kisomi zitasaidia kutupa upeo wa kulinda mazingira ya nchi yetu na nchi tatu zilizomo katika mradi huu," Dk Gwamaka. Alisema kuwa tafiti za kisomi ni muhimu na itaongeza uelewa miongoni mwa washiriki.Dk Gwamaka alisema kama wadau watakubaliana basi uchimbaji wa urana, utakuwa na manufaa kwa nchi zote husika na hasa kwa kuwa urani inatoa mchango mkubwa katika kuzalisha umeme. Warsha ya aina hiyo inafanyika pia katika nchi za Malawi, Namibia na Zambia, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa lengo la kuwa na uchimbaji, uchakataji, usafirishaji na matumizi salama ya urana.Wajumbe walitoka Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Wizara ya Madini na NEMC, taasisi mbalimbali za umma na binafsi, zinazojishughulisha na madini pamoja na mazingira. Nchini Tanzania, Chuo Kikuu cha Dodoma, ndicho kinachoratibu na kukusanya taarifa zitakazotoa majibu iwapo ni busara na ni namna gani urani ichimbwe hapa Tanzania au vinginevyo.Washiriki katika warsha hiyo walijadili changamoto zinazojitokeza katika uchimbaji wa madini, hasa urani kwa sababu urani ni madini yenye madhara makubwa kwa viumbe na mazingira na hasa kama uchimbaji unafanywa kabla ya utafiti wa kutosha. Mkuu wa Kitivo cha Sayansi Mazingira na Teknolojia wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Dk Meserecordias Lema alisema washirika walipata nafasi ya kujadili namna bora ya kuboresha sheria ili ziendane na sheria za nchi husika."Warsha hii ililenga kutafuta njia bora ya kufanyia maboresho ya sheria katika uchimbaji wa urani kusudi mataifa yote manne yawe na mfumo wa sheria mmoja ili kuondokana na madhara ya urani katika nyanja mbalimbali," Dk Lema alisisitiza. Alisema wajumbe walijikita katika ulinzi na usalama kwenye uchimbaji, uchakataji na usafirishaji na matumizi salama ya urani.
3
USIMAMIZI mbovu wa sekta ya madini nchini ni moja ya sababu, zilizofamfanya Rais John Magufuli kufanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.Katika mabadiliko hayo juzi, Rais Magufuli alimteua Doto Biteko kuwa Waziri wa Madini na kumuondoa aliyekuwa Waziri wa wizara hiyo, Angella Kairuki, aliyemteua kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, wizara ambayo ni mpya.Rais Magufuli alitoboa siri ya mabadiliko hayo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, alipowaapisha viongozi mbalimbali waliopata uteuzi hivi karibuni akiwemo Biteko, makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu na makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma.Siri ya kumteua BitekoAkielezea ni kwanini amemteua Biteko kuwa Waziri wa Madini, Rais Magufuli alisema ni kutokana na Spika wa Bunge, Job Ndugai, kumwamini Biteko kwa kumteua kuongoza Kamati ya Nishati na Madini na baadaye kumteua kuongoza Kamati ya kuchunguza wizi wa madini nchini, hivyo kumshawishi kumteua kuwa Naibu Waziri na kisha Waziri kamili wa Madini.Alisema alikuwa akifuatilia kwa nini kila mara Spika alikuwa akimteua Biteko kwenye mambo yanayohusu madini, ndipo alibaini kuwa utendaji kazi wake katika nafasi zote alizoteuliwa kuongoza, ulikuwa mzuri na yeye akaamua kumteua.“Mheshimiwa Spika, ulipounda kamati za Bunge ulimteua Biteko kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, ulipounda tena Kamati ya kufuatilia Madini yanavyoibwa, ulimteua tena Biteko kuwa Mwenyekiti, nami nilikuwa namfuatilia, nikaamua kumteua,” alieleza Rais Magufuli.Alimtaka Biteko achape kazi, kwa vile hatasita kumuondoa, kwa kuwa dhana yake ya kuendelea kufanya mabadiliko kwa watendaji wake, bado iko palepale.Alisema rasilimali zilizopo nchini ni lazima ziwanufaishe wananchi, hivyo asiporidhika na utendaji wa viongozi anaowateua, hatasita kuwaondoa.Akerwa usimamizi wa madiniRais Magufuli alisema pamoja na kutungwa kwa Sheria inayosimamia Sekta ya Madini, lakini cha kusikitisha ni kwamba bado kuna udhaifu mkubwa katika Wizara ya Madini, kwa kushindwa kusimamia sekta hiyo vizuri kwa manufaa ya Taifa.Kwa mujibu wa Rais Magufuli, ripoti iliyomfikia hivi karibuni, inaonesha kuwa Tanzania si nchi inayoongoza kwa kuuza dhahabu nje ya nchi katika Afrika Mashariki, licha ya kuongoza kuwa na dhahabu nyingi katika ukanda huo.Alisema Wizara ya Madini imeshindwa kuwasimamia wachimbaji wadogo wa madini nchini ;na ndiyo maana hajui ni wapi wachimbaji hao wanauza madini yao.Alisema ni wajibu wa Wizara hiyo, kujua ni wapi wachimbaji wadogo wanauza madini yao, soko la dhahabu lilipo na Taifa linapaswa kunufaika vipi.“Sheria ya madini imeweka utaratibu mzuri wa kusimamia madini ikiwemo masuala ya mikataba na namna wachimbaji wadogo wanavyoweza kushiriki kuchimba na kuuza madini.“Lakini cha kusikitisha dhahabu haiinufaishi Tanzania licha ya Wizara kujaa watendaji wote wanaotakiwa,” alieleza Rais Magufuli.Maagizo mapya kwa wizara, BOTKutokana na udhaifu huo, Rais Magufuli alimwagiza Waziri Biteko kuhakikisha anaanzisha Vituo Maalum vya Kuuzia Madini (Mineral Centres) nchini, kama Sheria ya Madini inavyotaka.Alimtaka Biteko pia kushirikiana na Wizara ya Fedha kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ili ianze kununua dhahabu ili kuwa na akiba ya madini hayo, kwa kuwa dhahabu ni fedha.“Kaanze na vituo vya kuuzia madini kama kule Geita, Mwanza, Shinyanga, Mirerani na kwingineko; vituo hivi vitatusaidia kujua kiasi cha madini tunachouza kwa mwaka, lakini pia wachimbaji wadogo wataweza kuchangia mapato kwa kuuza madini yao kwenye vituo hivi,” alisisitiza Rais Magufuli.Awaunganisha Waziri Ummy, Dk Chaula kiainaKatika hatua nyingine, Rais Magufuli alieleza namna alivyoamua kuwapanga katika wizara moja, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu aliyekuwa na mzozo na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Tamisemi, ambaye sasa amemteua kuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ya Afya, Dk Zainabu Chaula.Kwa mujibu wa Rais Magufuli, japo viongozi hao wawili wote wanatoka Tanga, walikuwa hawaelewani na ndiyo maana akaamua kumteua Dk Chaula kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ili wakae wizara moja na Waziri Ummy, kama njia ya kuwapatanisha ili waweze kuchapa kazi kwa bidii.Alisema katika utekelezaji wa miradi ya afya, ambapo Wizara ya Afya inashirikiana na Wizara ya Tamisemi, viongozi hao wawili wamekuwa wanatofautiana na kutumiana meseji za ugomvi, hatua iliyomfanya ampandishe Dk Chaula kuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Afya ili wafanye kazi kwa pamoja, kama njia ya kuwapatanisha.Uteuzi wa Dk Mpoki kuwa BaloziKuhusu uteuzi wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, DK Mpoki Ulisubisya kuwa Balozi, Rais Magufuli alisema ni kutokana na kiongozi huyo kusafiri nje ya nchi mara kwa mara.Alisema baada ya kufuatilia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dk John Kijazi kuhusu namna viongozi wanavyosafiri nje, alibaini Dk Mpoki kuomba vibali mara nyingi zaidi ili kusafiri nje na kuona anafaa kuendelea kuitumikia nchi akiwa huko huko nje kwa nafasi ya Balozi.Viongozi wengine alioeleza bila kuwataja majina kuwa wanalumbana ni Mkuu wa Wilaya ya Nyasa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Gairo na Mbunge wa Jimbo hilo, huku akisema kuwa malumbano yaliyokuwepo kati ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na Mkuu wa Wilaya, yamekwisha baada ya yeye Rais kuwatumia ujumbe maalumu.Viongozi walioapishwa Viongozi walioapishwa jana mbali ya Biteko na Dk Chaula ni Elius Mwakalinga, ambaye amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.Kabla ya uteuzi huo, Mwakalinga alikuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) na anachukua nafasi ya Joseph Nyamuhanga, aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Tamisemi.Mwingine ni Dorothy Mwaluko aliyeapishwa kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera na Uwekezaji na kabla ya uteuzi huo, alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.Pia Rais Magufuli alimwapisha Dk Dorothy Gwajima kuwa Naibu Katibu Mkuu Tamisemi anayeshughulikia Afya. Kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkurugenzi wa Tiba wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.Naibu Katibu Mkuu mwingine aliyeapishwa ni Dk Francis Michael, ambaye amekuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Kabla ya uteuzi huo, Dk Michael alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Aliyekuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu, Profesa Faustin Kamuzora, aliapishwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Kagera kuchukua nafasi ya Athumani Diwani, aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).Waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika Ndugai, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Naibu Spika Dk Tulia Ackson, mawaziri, naibu mawaziri na viongozi mbalimbali wa serikali na viongozi wa dini
3
MHASIBU wa Klabu ya Simba, Amos Gahumeni (39) ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu namna washitakiwa Evans Aveva na wenzake walivyotumia fedha za mauzo ya mshambuliaji wa klabu hiyo, Emmanuel Okwi.Gahumeni ambaye ni shahidi wa sita katika kesi hiyo ya utakatishaji fedha alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa.Akiongozwa na Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai, shahidi huyo alidai aliajiriwa na klabu hiyo mwaka 2014 na kwamba kazi yake ni kuandaa malipo, taarifa za fedha na bajeti ya mwaka.Alidai Machi 14, 2016 kuliitishwa kikao cha kawaida cha Kamati Tendaji ambacho kilikuwa na ajenda 10 na ajenda namba saba ilihusu taarifa ya mauzi ya mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Uganda, the Cranes. Alidai fedha ambayo iliingia kwenye akaunti ya klabu hiyo ni Dola za Marekani 319,212 baada ya Okwi kuuzwa kwenye timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia.“Baada ya kutoa taarifa hiyo waliamua fedha hizo zitumoke kwenye ujenzu sa uwanja wa Simba uliopo Bunju, pia Dola za Marekani 17,000 alipwe Zacharia Hanspope na nyingine zifunguliwe akaunti maalumu kwa ajili ya uwanja huo,” alidai Gaubeli.Pia alidai siku iliyofuata, akiwa ofisini kwake aliyekuwa makamu wa rais wa klabu hiyo, Godfrey Nyange alimuomba kitabu cha benki cha dola ambacho kina akaunti iliyopokea fedha za mauzo ya Okwi.Alidai kuwa alimpatia mshitakiwa huyo wa pili, ambaye aliondoka na kitabu hicho na alipokirudisha hakikuwa na karatasi mbili na pia alimkabidhi karatasi kutoka Benki ya CRDB cha kuhamisha fedha ambazo ni Dola za Marekani 300,000 kwenda kwenye akaunti ya Aveva.
4
Azam FC usiku wa kuamkia leo iliibuka na ushindi wa mabao 3-1, dhidi ya KMC katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Azam Complex Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.Akizungumza na gazeti hili Kocha huyo alisema kuwa jitihada zao zote kwa sasa wamezielekeza kwenye michuano hiyo baada ya nafasi finyu waliyokuwa nayo kweye ligi kutokana na kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo.“Hatujakata tamaa na ubingwa wa Tanzania Bara, lakini nafasi tuliyopo na timu ambazo zipo juu yetu inatupa wakati mgumu ndiyo maana nimewaambia wachezaji wangu kuhakikisha tunacheza kwa nguvu na kutwaa ubingwa wa Kombe la FA mwaka huu kwa sababu ndiyo sehemu pekee itakayoturudisha kwenye michuano ya kimataifa mwakani,” amesema Cioaba.Mromania huyo alisema anajua kadri wanavyosonga mbele kwenye michuano hiyo ndiyo wanakutana na timu ngumu lakini hilo siyo kikwazo kwao wamejipanga kukabiliana na timu yoyote watakayopangiwa nayo kitu cha msingi kwao ni ubingwa.Alisema mbali na Azam kutaka kurudi kwenye michuano ya kimataifa mwakani lakini kitu kingine ni kutaka kuingia kwenye rekodi ya kuwa moja ya timu ambayo imelitwaa taji hilo baada ya Yanga na Simba ambazo zimefanya hivyo kwa miaka miwili iliyopita tangu kurudishwa kwa michuano hiyo.Azam ipo nyuma kwa pointi saba dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba, wenye pointi 42 na pointi mbili dhidi ya mabingwa watetezi, Yanga waliopo nafasi ya pili na yenyewe inashika nafasi ya tatu kwa kumiliki pointi 35 huku ikiwa mbele kwa mchezo mmoja dhidi ya timu hizo mbili za juu.
4
    Na ELIZABETH HOMBO-DAR ES SALAAM SIKU chache baada ya wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Halima Mdee (Kawe) na Esther Bulaya (Bunda) kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa mwaka mmoja, Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu, amesema watakwenda mahakamani. Mdee na Bulaya walikumbana na kifungo hicho mwanzoni mwa wiki baada ya kukutwa na kosa la kudharau mamlaka ya Spika wa Bunge, Job Ndugai. Kutokana na hukumu hiyo, Lissu ambaye pia ni mwanasheria mkuu wa Chadema, ameliambia MTANZANIA jana kwamba ana mpango wa kukutana na wabunge hao kuandaa hoja ya kupeleka Mahakama Kuu. Alisema kusudio la kupeleka Mahakama Kuu hoja ya utetezi wa wabunge hao, ni kupata tafsiri ya uamuzi aliouchukua Spika Ndugai na kwamba utaratibu huo hawatakubaliana nao kwa vyovyote vile. Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema uamuzi aliouchukua Spika Ndugai wa kufungia wabunge hao kuhudhuria vikao kwa miezi kumi, ni makosa makubwa. “Tunataka mahakama ituambie kwenye ‘judicial review’ je, Bunge linaweza kufuta ubunge wa mbunge wake, kama wanavyotafsiri hawa kina Ndugai? Je, Bunge linaweza likatoa adhabu hata nje ya adhabu iliyopo kwenye kanuni? Je, Bunge lina uwezo wa kumwadhibu mbunge bila kumpa fursa ya kujitetea kwenye kamati na Bunge lenyewe. “Tutaomba Mahakama Kuu itupe tafsiri, kwa vyovyote vile utaratibu huu hatutakubaliana nao, tukienda hivi, hawa CCM wa bungeni kuna siku wataamua mbunge asiingie bungeni kwa miaka mitano halafu wanasema Bunge lina mamlaka lisiingiliwe, Bunge halina mamlaka hayo. “Kuna kanuni za kutoa adhabu kwa mbunge yeyote anayefanya kosa. Adhabu ya kumfungia mbunge kwa miezi 10 haipo kwenye Kanuni za Bunge la Tanzania, lakini kumekuwa na tabia na utamaduni, sasa inapofika kwa wabunge wa upinzani wanapewa adhabu kubwa kubwa ambazo ziko nje kabisa za utaratibu wa kanuni zilizopo,” alisema. Alisema sheria na kanuni za Bunge imesema adhabu ya mbunge ni kumfungia vikao 20 kwa maana ya siku na kwamba adhabu nyinginezo haiwezi ikawa kifungo cha siku 100 au miezi kumi. Alisema tafsiri nyinginezo si kuzuia tena kuhudhuria vikao kwa siku 20, bali inaweza ikawa kumnyima mbunge huyo mshahara, kuzuia bima yake ya afya, kumfutia posho ya jimbo. “Sasa Bunge la Ndugai wanaelekea kufikiria kwamba Bunge lina uwezo wa kumsimamisha mbunge kuhudhuria vikao vya Bunge kwa kipindi chochote kile watakachoamua wao. Hiyo tafsiri ni ya makosa kabisa ya mamlaka ya kutoa adhabu ya Bunge." alisema.
3
MAREGESI PAUL Na RAMADHAN HASSAN -DODOMA MBUNGE wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), amesema wananchi wamewageuza wabunge wa Tanzania na kuwa kama mashine za kutolea fedha (ATM) na Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS). Kutokana na hali hiyo, amesema kuna haja Serikali kuboresha mafao yao ili yaendane na majukumu wanayokabiliana nayo. Waitara aliyasema hayo jana mjini hapa wakati wa semina ya wabunge walioko katika mabunge ya nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CPA). “Mshahara wa mbunge kila mwezi unakatwa shilingi milioni 1.2, lakini baada ya kumaliza miaka mitano ya ubunge, mafao yake yanakatwa tena. “Hivi huo utaratibu mliutoa wapi wakati haupo nchi yoyote duniani? Sisi wabunge tumegeuzwa kama ATM au saccos kwa sababu tutatoa pesa kila mahali. “Kule Kenya ofisi ya mbunge ni kama taasisi kwa sababu ina mbunge na ina mtafiti anayemsaidia mbunge kila anapotaka kufanya mambo yake. "Hata kukiwa na harambee, mbunge unaitwa na kutakiwa uchangie fedha nyingi, sasa utachanga kwa fedha zipi wakati mnatulipa kidogo, yaani huu ni mzigo kwetu wabunge. “Kwa hiyo, tuongezeeni mafao kwa sababu tunalipwa kidogo sana ikilinganishwa na nchi zingine,”alisema Waitara. Kwa upande wake, Mbunge wa Songwe, Philipo Mulugo (CCM), pamoja na kulalamikia mafao madogo, alitaka kujua takwimu halisi za malipo wanayolipwa wabunge wa Kenya na nchi zingine ili wayalinganishe na wanayolipwa wabunge wa Tanzania. Naye Mbunge wa Viti Maalum, Shally Raymond (CCM), alisema kuna haja kwa wabunge hao kuboreshewa mafao yao ili waweze kufanya kazi kwa mafanikio zaidi. Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema), pamoja na kulalamikia mafao, alilalamikia utaratibu wa vyama vya siasa kukutanisha wabunge wao ili wakubaliane kupitisha mambo yenye masilahi ya chama badala ya kuangalia utaifa. Wakati hao wakisema hayo, Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), alitaka wabunge wawekewe bima ya afya ya maisha kama sheria inavyotaka. “Kwanza kabisa nimeshangaa kusikia makao makuu ya CPA Barani Afrika yapo Tanzania na pia ofisi yao iko hapa bungeni. “Kuhusu hilo suala la bima ya afya ya maisha ya wabunge, nashangaa kwanini Serikali haitaki kuliruhusu kwa wabunge kwani hata Tume ya Utumishi ya Bunge, imekuwa ikisisitiza juu ya jambo hilo. “Yaani Tume ya Utumishi imelifuatilia kwa muda mrefu, lakini Serikali haitaki kukubali, jambo ambalo hakitendi haki kwa sababu baadhi ya wabunge wameshafariki na wengine wamepata ulemavu,” alisema Lugola. Hata hivyo, wakati akijibu hoja hizo, Katibu wa Spika wa Bunge, Said Yakub, alisema chanzo cha wabunge kugeuzwa ATM ni wao wenyewe kwa sababu ndivyo walivyowazoesha wapiga kura wao.
3
MAMLAKA ya hali ya hewa nchini imetoa tahadhari kwa kaya 48,000 zinazoishi katika maeneo hatarishi kuwa zipo katika hatari ya kupata madhara makubwa kutokana na mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha mwezi huu.Kutokana na tishio hilo, inakadiriwa kuwa serikali inahitaji kiasi cha faranga trilioni 1.4 kuhamisha kaya hizo kwenda maeneo salama. Mamlaka ya Nyumba Rwanda (RHA) imeeleza kukosa rasilimali za kuzipatia makazi kaya hizo kutokana na gharama inayotakiwa kuwa kubwa. Inaelezwa utabiri wa hali ya hewa wa Machi mpaka Mei mwaka huu unaonesha kutakuwa na mvua kubwa kwa baadhi ya majimbo ya Magharibi, Kaskazini na Kusini mwa nchi hiyo, hivyo kusababisha majanga mbalimbali.Mkurugenzi Mkuu wa RHA, Eric Serubibi, alisema kuna zaidi ya kaya 48,000 zinazoishi katika mazingira hatarishi nchini humo na kati yao kaya 13,000 zikiishi jijini Kigali. Serubibi alieleza kuhamisha kaya moja kutoka maeneo hayo kwenda maeneo salama yenye nyumba, barabara, maji, nishati na miundombinu stahili unatakiwa kuwa na faranga milioni 30. RHA imeanza kutekeleza mipango ya pamoja Kigali na wadau mbalimbali kuwaondoa watu kutoka maeneo hatarishi ya Rebero, Jali, Kimisagara na maeneo mengine ya Kigali.
3