text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
KLABU ya Liverpool imeomba kuvaa beji zao mpya za dhahabu walizopata baada ya kutwaa Kombe la Dunia la Klabu la FIFA kwenye mechi za Ligi Kuu England.Sheria za Ligi Kuu England zinasema kuwa, ujumbe wa hisani tu ndio unaweza kuongezwa kwenye jezi katikati ya msimu wa Ligi Kuu na kitu chochote tofauti na hicho lazima kiridhiwe na bodi ya ligi.Lakini Liverpool wameuliza ikiwa beji hizo zinaweza kuvaliwa katika mechi zao zote na kwamba itaonyesha mpira wa miguu kwenye muonekano mzuri, limeandika gazeti la The Athletic. Viongozi wa klabu hiyo wanaamini kuchukua ubingwa wa dunia ni mafanikio makubwa, hivyo Liverpool inapaswa kuwa na haki ya kuivaa beji hizo katika mashindano yote.Real Madrid - ambao walikuwa mabingwa wa dunia 2016, 2017 na 2018, walipewa ruhusa ya kuvaa beji kwenye ligi ya La Liga. Hata hivyo, Liverpool wataruhusiwa kuvaa beji hizo kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya Februari 18 dhidi ya Atletico Madrid. Ili kuvaa beji hizo kwenye Kombe la FA, Liverpool italazimika kupeleka maombi kwa Shirikisho la Soka watakapo ikaribisha Everton katika mzunguko wa tatu Januari 5 mwakani.Manchester United walikataliwa kuvaa beji zao kwenye Ligi Kuu baada ya kushinda Kombe la Dunia la Klabu la FIFA mwaka 2008. Miongozo ya sasa ya FIFA inasema kwamba beji iliyoletwa mwaka 2007 inaweza kutumika tu kwenye jezi za viongozi wa timu na haiwezi kutumiwa kwenye toleo la zamani au jezi za timu za mazoezi, trakisuti, bipsi au bidhaa nyingine.Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp, anasema kwa mujibu wa sheria za FIFA, wanaweza kuvaa beji hizo hadi fainali ya Kombe la Dunia la Klabu la 2020. Liverpool imetwaa Kombe la Dunia la Klabu baada ya kuifunga Flamengo ya Brazil kwa bao 1-0, lililofungwa na Roberto Firmino kwenye muda wa nyongeza Jumamosi iliyopita. Ni taji la tatu la Liverpool kwa mwaka huu, likiwamo la Ligi ya Mabingwa na Super Cup Ulaya. | 4 |
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Othman Dunga juzi, alipokuwa akitoa maelezo ya utoaji wa mikopo ya power tiller wilayani humo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Omar Kwaang’ aliyemwakilisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk Mary Nagu.Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Pahi wilayani Kondoa, Dunga alisema idadi hiyo ya wakulima 600 wanaohitaji mikopo ya matrekta hayo madogo ni ya awamu ya pili ya utoaji wa mikopo hiyo.Alisema kwa msimu huu wa kilimo wa 2013/2014, kampuni hiyo imeingiza nchini zaidi ya power tiller 70 zenye thamani ya Sh milioni 315 katika Wilaya ya Kondoa, ambapo wakulima wameweza kulima kwa wakati na kwa muda mfupi tofauti na kilimo cha kutumia jembe la mkono au wanyama kazi.“Pamoja na kuwasaidia katika kilimo, power tiller imewawezesha wakulima kubeba mizigo mashambani baada ya mavuno. Pia zimekuwa zinawasaidia katika kubeba mahindi, kusaga nafaka na kumwagilia maji katika bustani na mashamba madogo,” alisema.Kuhusiana na waombaji hao wapya wa mikopo, Dunga alisema kampuni hiyo inaandaa utaratibu, utakaowawezesha kupata matrekta hayo madogo haraka ili kuwawezesha kutimiza ndoto zao za kuondokana na kilimo cha jembe la mkono na kukuza pato lao kutokana na kuingia kwenye kilimo chenye tija.“Kampuni inawaahidi wakulima kuwa itakuwa bega kwa bega nao kwani kilimo ndiyo mhimili wa uchumi katika Taifa,” alisema Dunga.Kwa upande wake, Kwaang’ alisema kampuni hiyo imekuwa mkombozi kwa wakulima kutokana na kujibu kwa vitendo maombi ya wakulima katika kuwapa pembejeo na zana za kisasa za kilimo kila wanapopokea maombi hayo na kwa wakati.Mbali ya Kondoa, tayari kampuni hiyo ya Farm Green imesambaza matrekta madogo ya power tiller katika Wilaya za Kiteto, Manyoni, Nkasi, Kahama, Chato, Kwimba, Mtwara Mjini na Iramba, ambapo wakulima wameweza kubadili aina yao ya kilimo na kuingia katika kilimo chenye tija. | 5 |
Alisema wastaafu hao wamefaidika na mfuko huo hivyo kwa hivi sasa wamejipanga kutoa elimu zaidi ili mpango huo uweze kueleweka kwa wastaafu na wastaafu waajiriwa.Ofisa huyo alisema mikopo hiyo ambayo imekuwa ikitolewa kupitia Benki ya Posta imelenga kuwawezesha wastaafu kukidhi mahitaji halisi ya kifedha.“Mahitaji hayo ni pamoja na gharama za matibabu, ukarabati wa nyumba, kusomesha watoto na ndugu, biashara au miradi mbalimbali na pia kuboresha maisha yao,” alisema.Alitaja mojawapo ya kigezo kinachotakiwa kwa wastaafu hao ili waweze kupata mkopo huo ni kuridhia kupitisha malipo yao ya pensheni ya kila mwezi kwenye Benki ya Posta Tanzania ambapo utaratibu wa marejesho umewekwa baina ya pande zote mbili.Tineishemo alisema wamekuwa wakitoa mkopo kuanzia Sh 500,000 hadi Sh milioni 20 kutegemea na kiwango cha pensheni ya mwanachama, huku wakitakiwa kuirejesha kati ya mwaka mmoja hadi mitatu.Alisema matarajio yao ni kutoa mikopo kwa wastaafu 1000 kila mwaka, ambapo kwa sasa wamejipanga kutoa elimu zaidi ili mpango huo uweze kueleweka kwa wastaafu na wastaafu watarajiwa.Kuhusu changamoto alisema pamoja na kuwa na mwitikio mkubwa wa wastaafu kukopa, kutofautiana kwa viwango vya mishahara inayozaa mafao makubwa baadaye imesababisha wengine kushindwa kupata fedha kubwa wanayoihitaji. | 5 |
WANARIADHA kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wamefanikiwa kushinda katika Mashindano ya wazi ya riadha ya kilomita 10’The Greath Health Arusha Run’ yaliyofanyika jana hapa.Wanaume waliokimbia kilomita 10 Faraja Lazaro aliibuka mshindi kwa kutumia muda wa dadika 28:56:77 akifuatiwa na Joseph Panga wote kutoka JWTZ kwa muda wa dakika 28:01:57 na nafasi ya tatu kushikiliwa na Mathayo Sombi kutoka Talent kwa muda wa dakika 29:26:66.Wanawake Cecilia Panga alimaliza kwa muda wa dakika 33:42:14 akifuatiwa na Iscah Cheruta kutoka Kenya kwa dakika 34:58:28, huku nafasi ya tatu ikienda kwa Asha Salum kutoka JWTZ muda wa 35:02:43.Kocha Mkuu wa riadha katika JWTZ, Anthony Mwingereza amesema mafanikio yote ni chini ya usimamizi mahiri wa mazoezi kwa wanariadha hao na kusema hivi Sasa wanariadha hao wanajiandaa na Michezo ya Majeshi kwa nchi za Afrika Mashariki yatakayofanyika jijini Nairobi, Kenya mwezi ujao.Zaidi ya washiriki 800 kutoka ndani na nje ya mkoa Arusha walishiriki mbio hizo za kilomita 10, kilometa 2.5 kwa watoto na kilometa 5 kwa walemavu ikiwa ni mwaka wa tatu kufanyika zikilenga kuhamashisha cchezo wa riadha sambamba na upimaji afya kwa hiari .Katibu wa Chama Cha Riadha Tanzania (RT) Wilhelm Gidabuday alisema mbio zimeenda sawa licha ya kuwepo kwa baadhi ya watu ambao ni viongozi ndani ya chama waliotaka kuzihujumu mbio zisifanyike lakini wamejulikana na watachukuliwa hatua kali iwe fundisho kwa wote wenye kukwamisha riadha.“Nampongeza mwandaaji wa mbio hizo Dokta Kylie Gyubi kwa kufanikisha kufanyika sambamba na kuimarisha afya chama kitaangalia ratiba ili mbio hizo zisigongane tarehe na mbio za Bagamoyo ,”amesema Gidabuday.Washindi mbalimbali walizawadiwa zawadi za fedha na medali ambapo mshindi wa kwanza kwa wanawake na wanaume watakaokimbia kilomita 10 alijipatia shilingi 500,000, mshindi wa pili alipata 300,000, mshindi wa tatu alipata 100,000 na kuanzia mshindi wa nne hadi wa kumi atapata 50,000 kila mmoja.Zawadi kwa walemavu waliokimbia kilomita 5 mshindi wa kwanza kwa wanawake na wanaume alijinyakulia shilingi 200,000, mshindi wa pili 150,000, mshindi wa tatu 100,000.Kwa upande wa watoto kilomita 2.5 mshindi atapata shilingi 100,000, mshindi wa pili 80,000, mshindi wa tatu 60,000 . | 4 |
Ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mechi za raundi hiyo zitachezwa kuanzia Februari 26 mpaka Machi mosi mwaka huu kwenye viwanja mbalimbali nchini.“Michuano ilishirikisha timu 64 kutoka Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili, inaingia katika mzunguko wa nne huku kukiwa na timu kutoka katika ngazi zote za ligi za TFF, jambo ambalo linamaanisha kuwa kuna ushindani wa kutosha,” alisema Kizuguto.Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Februari 26, Ndanda FC watawakaribisha JKT Ruvu katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara, huku Coastal Union wakiwa wenyeji wa wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.Februari 27, Mwadui FC watawakaribisha Rhino Rangers kwenye uwanja wa Mwadui Complex Shinyanga na Tanzania Prisons watacheza na mshindi kati ya Mbeya City/ Wenda FC kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.Februari 28, michezo mitatu itachezwa ambapo Simba watawakaribisha Singida United katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Panone FC watacheza dhidi ya Azam FC Uwanja wa Ushirika, Moshi huku Toto African wakicheza na Geita . | 4 |
MSHAMBULIAJI wa Simba, Emmanuel Okwi ameahidi kutoa raha katika tamasha la Simba linalotarajiwa kufanyika Agosti 8 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Simba hufanya tamasha lao Agosti 8 ya kila mwaka ambapo hucheza hutambulisha jezi watakazotumia msimu mzima, wachezaji na mwisho hucheza mechi ya kirafiki na timu kutoka nje ya nchi.Katika ujumbe wake alioutuma jana akiwa kwenye kambi ya maandalizi ya msimu na timu yake Uturuki, Okwi alisema wanaendelea vizuri na mazoezi kuhakikisha wanatoa burudani ya kipekee siku hiyo.“Tuko poa, mambo yanakwenda vizuri kwa ajili ya tamasha la Simba, tunajipanga kupambana ili kutoa burudani kwa mashabiki wetu kabla ya kuanza kwa msimu,” amesema.Okwi amesema chini ya Kocha mpya Patrick Aussems anaamini watafanya vizuri kwani wachezaji wanaonekana kuwa na morali ya hali ya juu tayari kwa burudani. Kikosi hicho kinatarajiwa kuwasili nchini kuanzia Agosti 5, mwaka huu tayari kwa tamasha hilo.Hivi karibuni Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba Haji Manara alisema tamasha la mwaka huu litakuwa tofauti na misimu mingine wakipania kulifanya liwe kubwa na lenye kuvutia kwa burudani mbalimbali. | 4 |
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza ametoa ahadi hiyo wakati wa hafla ya kuikaribisha timu hiyo Australia iliyoandaliwa Dar es Salaam na Balozi wa nchi hiyo nchini Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.Shonza alisema kuwa Serikali ya Tanzania iko nyuma ya wachezaji hao, hivyo wasiwe na wasiwasi wowote kwani wanachotakiwa ni kushindana na kuipeperusha vizuri bendera ya taifa Australia.Michezo hiyo ya Jumuiya ya Madola itafanyika Gold Coast, Australia kuanzia Aprili 4 hadi 15 na Tanzania itapeleka timu za riadha, ngumi, kuogelea na mpira wa meza.Balozi wa Australia nchini Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda, Alison Chartres aliwakaribisha wachezaji hao, ambao alikula nao chakula cha mchana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania, TOC, Filbert Bayi aliwataja wanariadha watakaenda Australia kuwa ni Emmanuel Giniki (meta 5,000-10,000), Augustino Sulle, Said Makula, Magdalena Shauri, Stephano Huche na Sara Ramadhani (Marathon).Wengine ni Ali Hamisi Gulam (meta 100/200), Anthony Mwanga wakati makocha wa timu hiyo ni pamoja na Zakaria Barie na Lwiza John.Timu ya ngumi itakuwa na Kassim Mbutike, Selemani Kidunda, Ezra Paul na Haruna Swanga wakati kocha weao ni Mkenya Benjamin Oyombi. Timu ya kuogelea itakuwa na akina Hilal Hilal na Sonia Tumiotto wakati kocha wao ni Khalid Rushaka huku timu ya mpira wa meza inaundwa na Amon Tumaini, Masoud Mtalaso, Neema Mwaisula na Fathiya Pazi wakati kocha ni Ramadhani Suleiman.Viongozi watakaoongoza na timu hiyo ni pamoja na Mkurugenzi wa Michezo, Dk Yusuph Singo (Mkuu wa msafara), Nassra Mohamed (Meneja wa timu) na Joakim Mshanga (Daktari wa timu).Wengine kwa nafasi zao ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza, Rais wa TOC, Gulam Rashid, Bayi na Petro Kivike (Msaidizi wa Waziri Shonza). Timu ya Tanzania inatarajia kuondoka Machi 27 na kwa sasa timu ya riadha iko Arusha wakati ile ya ndondi na mpira wa meza ziko Mkuza Kibaha mkoani Pwani. | 4 |
Na ELIYA MBONEA-ARUSHA WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, amewaomba radhi akina mama kwa kutozingatia uwiano wa uteuzi wa wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA). Kauli hiyo aliitoa jana mjini hapa alipokuwa akizindua rasmi shughuli za bodi hiyo mpya iliyoteulewa hivi karibuni ikiwa na wajumbe wanaume 11 na mwanamke mmoja, hivyo kukamilisha idadi ya wajumbe 12. Akizungumza na wajumbe wa bodi hiyo na Menejimenti ya NCAA, Dk. Kigwangalla, alisema katika uteuzi huo alihakikisha anazingatia vigezo zaidi kutoka kwa wajumbe. “Najisikia aibu kwa sababu sikuweka mizania sawa, nakiri siku-balance, akina mama naomba mnisamehe. Wakati ujao tutazingatia vigezo ambavyo watu wa nje waliviona. “Nakiri kukosea, hata baada ya kuwatangaza nisingeweza tena kuivunja bodi. Hivyo ngoja twende na bodi hii kwanza japokuwa humu ndani pia yupo mwanamke,” alisema Dk. Kigwangalla. Bodi hiyo inayoongozwa Mwenyekiti Professa Abiud Kaswamila, ina mjumbe mwanamke mmoja, Professa Kaunde Sibuga kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine Morogoro (SUA). Akizungumzia uteuzi huo kwa upande wake, Prof. Sibuga alisema kwa kawaida wajumbe wa bodi huteuliwa na waziri mwenyewe kwa kutumia vigezo na sifa anazozijua yeye. “Kwa kweli hata mimi naweza kusema baada ya kuangalia orodha ya majina ya wajumbe nilishtuka kujiona niko peke yangu. “Lakini ukweli ni kwamba ukiwa kwenye bodi au kikundi chochote kilichopewa majukumu, cha msingi ni kufuata taratibu zilizopo kufanya kazi na kushirikiana na wajumbe na mejimenti iliyopo.,” alisema. Profesa Sibuga, alisema kwanza anayo faraja kubwa ya kuwa mwanamke kwenye bodi, huku akiahidi kutoa mawazo makini kwenye nafasi yake. Wajumbe wengine ni Brigedia Jenerali mstaafu Aloyce Mwanjile, Bakari Nampenya, Deogratius Pisa, Edward Nduleti, Freddy Manongi, Haruna Masebu, Humphrey Mniaichi, Jumanne Feruzi, Michael Kamazima, Mhandisi Peter Ulanga na Ruzika Mheto. | 3 |
NA TUNU NASSOR
SHAHIDI katika kesi inayomkabili Salum Njwete maarufu ‘Scopion’, Daktari wa Kitengo cha Upasuaji cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk. Amin Abdulrahman ameiambia mahakama kuwa Saidi Mrisho alitobolewa utumbo mwembamba.
Akitoa ushahidi mbele ya hakimu Flora Haule Dk. Abdulrahmani alisema Septemba 7, mwaka jana saa 12 alfajiri akiwa chumba cha upasuaji alipigiwa simu na kitengo cha dharura cha hospitalini hapo kumtaka kwenda kumhudumia mgonjwa wa dharura.
“Baada ya kumfanyia uchunguzi niligundua anahitaji kufanyiwa upasuaji kutokana na jeraha kubwa lililokuwa kushoto mwa tumbo lake lililokuwa na urefu wa sentimita 30 kutoka katika ngozi ya ndani ya tumbo lililotoboa utumbo mwembamba na mengine madogo ambayo yalishonwa na kitengo cha dharura,” alisema Dk. Abdulrahman.
Alisema alifungua tumbo na kuliziba tundu hilo kasha kufunga tumbo na kumpeleka wodi namba 13 na kumpa rufaa kwa wataalamu wa macho kuendelea na uchunguzi wa majeraha ya machoni. Kesi hiyo itatajwa tena Machi 8, mwaka huu.
| 3 |
Staa wa muziki nchini Tanzania Rajab Abdul Kahali ameonesha mabadiliko ya kuondoa utambulisho wake wa kusainiwa chini ya lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) Tofauti hiyo ilionekana kwenye ukurasa wa staa huyo wa wimbo wa Kwangwaru aliomshirikisha Diamond Platnumz, ambapo kilichoondolewa ni maelezo ya awali ya kuwa chini ya mkataba na lebo hiyo. Julai 31, 2019 Harmonize alikanusha kuondoka katika kundi la WCB, lakini tukio hili linathibitisha yanayoongelewa kuwa yana ukweli. Kwenye Bio za wasanii wote waliopo chini ya Kundi la WCB (Rayvanny, Mbosso na Queen Darleen) zinasomeka “Singed under WCB Wasafi Label” isipokuwa Harmonize ambaye ameonekana kubadilisha hivi karibuni. Kwa sasa profile ya Harmonize inasomeka “East African Young Star 🇹🇿 #WCB4LIFE Booking: Bookharmonize@yahoo.com”, while the other read “Musician from East Africa Tz, Signed Under WCB wasafi Booking: Bookharmonize@yahoo.com”. Hivi karibuni, Harmonize almaarufu Konde Boy aliwaambia wanahabari waangalie masuala muhimu yatakayowezesha kukuza mziki wa Tanzania kuliko kutengeneza bifu kati yake na familia WCB. Wadadisi wa tasnia ya burudani nchini wanasema Konde Boy tayari amekuwa na jina kubwa kiasi cha kutotaka kuwa chini WCB ili kutengeneza pesa zaidi, hivyo kutaka kujitegemea. Julai mwaka ana Rich Mavoko alichukua uamuzi wa kujiondoa WCB, sababu ikiwa ni kutaka kujisimamia kazi zake yeye mwenyewe Muda utaeleza kama kweli Harmonize anaondoka au anabaki WCB!
| 1 |
Na AGATHA CHARLES
WATUMISHI wawili wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), wamekamatwa katika operesheni iliyofanywa na Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa kusaidia kupitisha kemikali bashirifu za ephedrine zinazotumika kutengenezea dawa za kulevya aina ya heroine.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Mamlaka hiyo zilizoko Upanga, Dar es Salaam, Kamishna wa Operesheni hiyo, Mihayo Msikhela, alisema pamoja na hao, wapo watumishi wengine wawili wa TRA ambao nyendo zao zinafuatiliwa.
“Wakati wa kukabidhiwa majina ya watu wanaojihusisha na dawa hizo nilitamka kuwa wapo watumishi wa umma wanaosaidia kuingiza hasa kemikali bashirifu,” alisema.
Kuhusu watumishi hao waliokamatwa ambao hata hivyo hakuwa tayari kuwataja kwa majina, alisema taratibu zinafanyika na wakati wowote watafikishwa mahakamani.
Kamishna Msikhela alisema tayari operesheni hiyo inayofanyika mikoa mbalimbali ya Tanzania bara kwa kukamata wasambazaji, wauzaji, watumiaji na kuharibu dawa za kulevya zilizoko mashambani, imeonyesha mafanikio ndani ya siku nne za mwanzo.
“Dawa za kulevya ziko katika makundi mawili, kundi la kwanza ni dawa za kulevya zilizoko mashambani na kundi la pili ni dawa za kulevya za viwandani. Na dawa za kulevya za mashambani kwa kiwango kikubwa ndio kero iliyopo kwa wananchi wetu. Matokeo haya ni operesheni ya siku nne tu hadi jana (Alhamisi),” alisema Kamishna Msikhela.
Alisema Mkoa wa Simiyu umeongoza kwa kuteketeza ekari 40 za bangi ukifuatiwa na Mkoa wa Kipolisi Tarime na Rorya kwa ekari 36 huku Lindi ukiongoza kwa kukamata dawa za viwandani aina ya heroine ambazo ni kete 50.
Kamishna Msikhela alitaja mikoa mingine iliyofanya vyema katika operesheni hiyo kuwa ni Tanga ambayo ilikamata mirungi kg 44, bangi puli 3, Morogoro (bangi kg 18, heroine kete 3), Shinyanga (bangi kg 10 na gramu 136), Kagera (bangi ekari 14, mirungi ekari 1), Njombe (bangi nusu ekari na gramu 20), Songwe (heroine kete 274, mirungi kg 3), Tabora (bangi kilo 6, mbegu kg 18), Singida (bangi misokoto 203, heroine kete 1), Rukwa (bangi kete 105), Mbeya (bangi kg 5), Kigoma bangi nusu ekari na Ruvuma bangi gramu 300.
Kamishna huyo alisema watuhumiwa hao ni wengi na wanaendelea kuhojiwa ambapo baadaye utafanyika utaratibu wa kisheria kuwafikisha mahakamani.
“Kama tutaendelea na mlipuko huu ambao umeongezewa mafuta, nina uhakika dawa za kulevya mashambani zinaweza kupungua kwa kiwango kikubwa. Tuunganishe nguvu na kuhakikisha vita hii inapiganwa kila sehemu,” alisema Kamishna Msikhela.
Akijibu swali la waandishi kuhusu kutaja na kushughulikia majina 97 wakiwemo wanaodaiwa kuwa ni vigogo na watoto wa vigogo, Kamishna Msikhela alisema kila aliyetajwa ataguswa.
“Yeyote aliyetajwa kwenye orodha hiyo ambayo ni orodha yenye fumbo ataguswa, hatutazami kwamba kigogo ni yupi na yupi si kigogo, yaliyomo mle ni majina ya wahalifu kama wahalifu wengine,” alisema Kamishna Msikhela.
Alisema orodha hiyo ambayo haina muda mrefu tangu ikabidhiwe kwao, ufuatiliaji umeanza na hivyo atatoa taarifa.
Akijibu swali lingine kuhusu orodha za awali zilizowataja kwa majina watuhumiwa huku ile ya majina 97 wakifichwa, Kamishna Msikhela alisema ni mfumo unaotumika.
“Ni mfumo uliotumika, yapo makosa ya mtaani hayaendelei kusumbua tena. Yapo makosa yaliyo wazi na yapo makosa yaliyojificha. Kwa hiyo yaliyo wazi tutajua yalikuwa katika hatua ipi na yaliyojificha yako kwenye hatua ipi na yanafanywa vipi,” alisema Kamishna Msikhela.
Kamishna Msikhela alisema:
“Vita ina mifumo mbalimbali ya upiganwaji, kwa hiyo mifumo yote itatumika ilimradi itakupelekea kwenye mafanikio na ukatoka umetangazwa you’re a hero (shujaa) yote huwa inatumika.”
Alisema vita ya dawa za kulevya ilianza miaka ya nyuma na kinachofanyika hivi sasa ni mwendelezo kama ilivyo upambanaji duniani kote.
“Huu ni mwendelezo kama ilivyo dunia nzima inavyopiganwa na sisi tunawajibika kupigana hii vita mpaka dunia itakapoweza kuipunguza kabisa au kuimaliza,” alisema Kamishna Msikhela.
Kamishna Msikhela alisema pamoja na Mamlaka hiyo iliyotangazwa hivi karibuni, lakini pia kuna vyombo vya ulinzi na usalama na hasa Jeshi la Polisi ambavyo utaratibu wa kuripoti na kufanya majukumu yake uko pale pale. | 3 |
Akizungumza na gazeti hili jana, Katibu Mkuu wa Magongo mkoa wa Dar es Salaam (DRHA), Mnonda Magani alisema mashindano hayo yatashirikisha timu za kiraia na wanafunzi wa shule za sekondari na msingi ambazo zilipatiwa elimu ya mchezo huo tangu mwaka uliopita.Alisema tayari timu kadhaa zimethibitisha ushiriki wao kwenye michuano hiyo zikiwemo TPDF timu mbili, Magereza, Kibasila Sekondari, Kigamboni, Juhudi Sekondari, Dar Calser timu nne, Dar Stars, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Nia Njema Sekondari na Makongo Sekondari.“Tumeamua kushiriki timu kuanzia shule za msingi, sekondari, vyuo na hata klabu za mtaani. Lengo ni kuwaleta pamoja kujifunza zaidi nini wengine wanachofanya, na kuleta ushindani wa timu na hata wachezaji ambao baadaye watakuwa ni lulu kwa timu ya taifa,” alisema.Magani alisema elimu waliyotoa mwaka jana imesaidia ushiriki mkubwa wa timu msimu huu na kwamba wanategemea kupata vipaji vipya ambavyo vitaongeza nguvu kwenye timu ya taifa.Alisema mipango ya maandalizi inaendelea vizuri katika kuhakikisha yanafanyika kwa usalama lakini pia wakiendelea na mikakati ya kutafuta udhamini kwa ajili ya kuunga mkono. | 4 |
JESHI la Polisi limejipanga vizuri katika ulinzi kipindi cha Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambao utahudhuriwa na wakuu wa nchi 16 Afrika.Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, msemaji wa jeshi hilo, David Misime alisema kuwa jeshi hilo limejiandaa kikamilifu kwa ajili ya ulinzi kwa siku za mkutano huo. Alisema jeshi limejiandaa kikamilifu kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa kuanzia ugeni utakapoingia nchini mpaka utakapomaliza mkutano na kuondoka.“Katika mkutano huo, shughuli mbalimbali zitakuwa zikiendelea kama vile wiki ya viwanda, mikutano ya awali pamoja na mkutano wenyewe wa wakuu wa nchi na serikali... jeshi la polisi limejipanga vizuri kwa ulinzi,” alisema.Alisema ulinzi huo ni katika kuhakikisha na kutekeleza majukumu yake ya kulinda maisha ya raia na mali zao pamoja na wageni wote watakaofika nchini. Misime alisema jeshi hilo pia linatoa wito kwa wananchi kuendelea kutii sheria za nchi ikiwemo sheria za usalama barabarani na pia kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi wanapotia shaka katika jambo lolote.Wakati huo huo, jeshi hilo limetoa taarifa ya ajali ya gari iliyoua askari wake watatu Julai 25 mwaka huu katika eneo la kijiji cha Kilimahewa barabara ya Kilwa wilaya ya Mkuranga.Kamanda Misime aliwataja askari waliopoteza maisha katika ajali hiyo kuwa ni Ofisa Mnadhimu Mkoa wa Kipolisi Rufiji, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Issah Bukuku, Inspekta Asteria wa ofisi ya Mkuu wa upelelezi Rifiji na askari namba G1132 Pc Lameck wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU). | 3 |
NA KULWA MZEE-DAR ES SALAAM ELIZABETH Balali ambaye ni dada wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, marehemu Daudi Balali, amekwamisha kesi inayomkabili kuendelea baada ya mshtakiwa pamoja na mdhamini wake kushindwa kufika mahakamani. Kesi hiyo ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, iliyokuja jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwa mshtakiwa kusomewa maelezo ya awali, ilikwama kwa sababu hakuwepo. Akiiwakilisha Jamhuri, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai kesi ilikuja kwa kusomwa maelezo ya awali, lakini mshtakiwa pamoja na mdhamini wake wote hawapo. Wankyo aliomba kesi hiyo iahirishwe hadi tarehe nyingine na endapo hatatokea mshtakiwa, upande wa Jamhuri utaomba hati ya kumkamata. Mahakama ilikubali kuahirisha kesi hiyo hadi Julai mosi, mwaka huu. Elizabeth aliwahi kukaa gerezani zaidi ya miezi sita, akikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi ambayo yalifutwa na kusomewa upya mashtaka ya kujipatia Sh milioni 25 kwa ulaghai. Anadaiwa kati ya Oktoba 19 na Desemba 21, 2017 Dar es Salaam alijipatia Sh milioni 25 kutoka kwa Dk. Roderick Kisenge kwa ulaghai. Inadaiwa alijipatia fedha hizo baada ya kujifanya anamuuzia eneo la mita za mraba 900 ambalo halijapimwa lililopo eneo la Boko Dovya, Kinondoni wakati akijua eneo hilo si lake. Alikana mashtaka na mahakama ilikubali kumpa dhamana kwa masharti ya kuwa na mdhamini mmoja, asaini dhamana ya maandishi ya Sh milioni tisa. | 3 |
Na FLORENCE SANAWA-MTWARA WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, ameagiza watumishi wa Serikali wanaokataa vyeti vya kuzaliwa vilivyoandikwa kwa mkono waanze kuvitambua. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, Dk. Mwakyembe alisema kitendo cha watumishi hao kukataa vyeti hivyo, wanakiuka sheria kwa kuwa Serikali inavitambua. “Mimi nashangaa kwa sababu kuna baadhi ya taasisi za Serikali zimekuwa zikikataa vyeti hivyo na kudai kuwa vimefojiwa, wakati si kweli. “Vyeti hivyo ni halali kwa sababu vina alama muhimu ambayo mtu yeyote hawezi kuifoji,” alisema Dk. Mwakyembe. Katika hatua nyingine, Dk. Mwakyembe aliyekuwa akimwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria, Profesas Palamagamba Kabudi, alisema hadi sasa Tanzania ipo nyuma katika usajili wa watoto ikilinganishwa na nchi nyingine duniani. “Ukijua idadi ya watu waliokwishafariki na walioko hai, inakurahisishia kujua kwa usahihi mahitaji na upungufu katika sekta mbalimbali ikiwamo afya, elimu na kwingineko. “Ukishayajua hayo, inakuwa rahisi kupanga mipango yako ya maendeleo kwa sababu utakuwa umeshajua mahitaji katika maeneo mbalimbali,” alisema Dk. Mwakyembe. Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini ( RITA), Profesa Hamis Dihenga, alisema bado uandikishaji wa vyeti vya kuzaliwa unahitaji hamasa zaidi ili kupunguza idadi ya wasiokuwa navyo. “Kwa mujibu wa sensa yetu iliyopita, bado Tanzania Bara ina asilimia ndogo ya watu waliojiandikisha kuchukua vyeti vya kuzaliwa ambao ni asilimia 13.4. “Lakini pia, asilimia 80 ya Watanzania hawana utambuzi wowote wa kisheria juu ya umuhimu wa kuwa na vyeti vya kuzaliwa,” alisema. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simu ya Mkononi ya TIGO, Simon Karikari, alisema katika usajili huo kwa mikoa ya Lindi na Mtwara, kampuni hiyo imetoa simu 1000 zitakazowawezesha watoaji wa huduma hiyo kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. | 3 |
WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha harambee ya kuichangia klabu ya Yanga itakayofanyika kwenye ukumbi wa Daimond Jubilee Dare es salaam.Mbali na mgeni rasmi huyo harambee hiyo pia inatarajiwa kuhudhuriwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete huku likinogeshwa na wasanii mbalimbali wa kizazi kipya ambao ni mashabiki wa timu hiyo.Harambee hiyo ya awamu ya pili iliyopewa jina la Kubwa Kuliko imeandaliwa kuratibiwa na kamati ya kuhamasisha wanachama na wapenzi wa timu hiyo inayoongozwa na mwenyekiti wake, ambaye ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Anthony Mavunde.Kwenye uzinduzi wa kampeni awamu ya kwanza iliyofanyika mkoani Dodoma iliyongozwa na kocha wa timu hiyo Mwinyi Zahera kamati hiyo ilifanikiwa kukusanya kiasi cha sh. Milion 500 kati ya kiasi cha Bilion 1.5 wanachotarajia kukipata.’Kubwa kuliko’ tukio linalotajwa litavunja rekodi kulishinda lile la awamu ya awali ambapo fedha takayopatikana itaisaidia timu hiyo kufanya usajili wa wachezaji wa maana kwa ajili ya kusuka kikosi kipya kwa ajili ya kuleta ushindani katika mechi za ligi ya ndani na kimataifa.Kwa mjibu wa mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya kuhamsisha wanachama na wapenzi kuichangia timu hiyo David Luhaga alisema maandalizi ya kuelekea kwenye tukio hilo kubwa yamekamilika hivyo amewaomba wanayanga kujitokeza kwa wingi kuunga mkono zoezi hilo.“Tunawaomba wanachama na wapenzi wajitokeze tumefanya maandalizi makubwa ikiwemo kuwaalika viongozi wakubwa kuchagiza tukio hili na kwa wale walioko mikoa mbalimbali waende kwenye matawi wakachangie tumeweka utaratibu makini wa kuhakikisha kila kinachotolewa kinatufikia,” alisema Luhaga. | 4 |
Viwango hivyo vimetangazwa siku moja baada ya Tanzania kupangwa katika Kundi G pamoja na timu za Misri, Nigeria na Chad katika kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017 nchini Gabon.Kwa mujibu wa viwango hivyo vya jana vya Fifa, Tanzania imeshuka kwa nafasi saba baada ya hivi karibuni kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Malawi ‘The Flames’ katika mechi ya kimataifa ya kalenda ya Fifa iliyochezwa Machi 29, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.Tanzania ni ya 30 kwa ubora Afrika wakati wapinzani wao kwa ajili ya Afcon 2017, Nigeria ni ya nane Afrika na 45 duniani, Misri ni ya 11 na ya 51 duniani na Chad ni ya 44 Afrika ikiwa ni ya 151 duniani.Uganda itakayocheza na Tanzania katika kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) Juni mwaka huu inaongoza kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ikiwa katika nafasi ya 72, Rwanda 74 na Ethiopia 101.Algeria bado inaongoza kwa Afrika wakati Djibouti ni ya mwisho kwa ubora katika nafasi ya 207 duniani.Kwa ujumla, Wales imechupa nafasi 15 hadi nafasi ya 22 kufikia nafasi yake hiyo ya juu zaidi. Baada ya kuwahi kushika nafasi ya 117 hivi karibuni mwaka 2011, Wales imeanza kupata mafanikio upya chini ya kocha marehemu Gary Speed.Brazil na Uruguay pia zimechupa, wakati Hispania na Uswisi zimerejea katika 10 bora badala ya Ufaransa na Italia.Aidha, Bhutan imechupa zaidi ikipanda nafasi 128 hadi nafasi ya 163.Katika hatua nyingine, Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Salum Mayanga amesema kitendo cha kupangwa kundi moja na miamba ya soka barani Afrika, Nigeria na Misri sio kitu cha kuogopwa isipokuwa wanahitaji kujipanga kuendana nao.Akizungumza na gazeti hili jana, Mayanga alisema baada ya kujua kundi lao, wanachotakiwa kuangalia ni uwezo wa kila timu kisha kujipanga mapema.“Tukishaangalia uwezo wa kila timu tunachotakiwa kufanya ni kujipanga kwa kuangalia mapungufu yetu yalipo, ili tutakapokuja kucheza tuendane na wao,” alisema kocha huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar.Mayanga alisema watu hawatakiwi kukata tamaa kwa kuangalia timu hizo, bali kwa kujipanga lolote linaweza kutokea.Alisema watajipanga na kwenda kucheza kwa ushindani wa hali ya juu katika kiwango kinachofanana na wao. | 4 |
LONDON, ENGLAND KOCHA wa zamani wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger, amefunguka kwa mara ya kwanza na kusema kuwa, anatarajia kurudi uwanjani mwanzoni mwa msimu wa 2019. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 69, amekuwa nje ya uwanja tangu alipoachana na Arsenal mwishoni mwa msimu uliopita, baada ya kuwa ndani ya klabu hiyo kwa kipindi cha miaka 22. Hata hivyo, kocha huyo ameweka wazi kuwa, ataonekana uwanjani, lakini si katika Ligi Kuu nchini England kama watu wanavyodhani. Alikuwa anahusishwa kutaka kutua katika klabu ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid. “Ninaamini mwanzoni mwa msimu wa 2019 nitaanza kuonekana viwanjani, kwa sasa nipo kwenye mapumziko mazuri, nimekuwa nikitumia muda mwingi kuangalia soka, lakini nimekuwa nikiongea mara kwa mara kwamba, ujio wangu hautakuwa kwenye Ligi Kuu England, kwa kuwa nimekuwa hapo kwa kipindi kirefu sana. “Hata hivyo, siwezi kuweka wazi kuwa nitakuwa kwenye timu gani, nitakuwa sehemu fulani lakini sijui ni wapi, muda ukifika kila kitu kitakuwa wazi,” alisema Wenger. | 4 |
.Dar es Salaam, Jumanne 17 Agosti 2019… Benki ya BancABC Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara leo imeendelea kudhihirisha ubunifu wake katika huduma zinazowanufaisha wateja wake baada ya kutangaza kuzindua akaunti mpya ya IZZE ambayo ni rahisi kufungua na haina makato yeyote ya mwezi.Kwa kupitia akaunti ya IZZE ya Bancabc, mteja anahitaji kuwa na kitambulisho cha taifa tu kilichotolewa na NIDA ili kufungua akaunti hiyo, na atapata riba hata akiwa na kianzio cha shilingi Elfu Kumi (Tshs10,000/-)Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua akaunti hiyo, Mkurugenzi wa Biashara na Wateja wadogo na wakati wa benki BancABC Joyce Malai alisema, ‘Leo kwenye soko la biashara watu wengi wanaangalia sehemu watakayo nufaika kuwekeza fedha zao na yenye uhakika wa kupata faida/manufaa kadhaa. Uhakika wa kupata faida au manufaa ni moja ya malengo muhimu kwa kila mtanzania. Vile vile, kufungua akaunti ya benki kwa siku hizi imekuwa ikichukuliwa kama hatua ngumu yenye kuhitaji muda na zaidi inaonekana kama inalenga watu wenye kipato kikubwa. Sisi BancABC tumelifanyia kazi suala hilo na ndio sababu tumekuja na akaunti ya IZZE ambayo ni rahisi kufungua kwani mteja anaweza kufungua akaunti hii hata kupitia mawakala wetu popote nchini’, Malai alisema.Malai aliongeza kuwa akaunti ya IZZE ni Rahisi kufungua kama ilivyo jina lake. Mteja anahitajika kuwa na kitambulisho cha taifa TU na haina kiasi chochote cha kuanzia, haina makato ya mwezi na muhimu zaidi ni kwamba mteja anapata riba kila mwezi ikiwa ana salio kuanzia shilingi elfu kumi (Tshs. 10, 000/-) au zaidi kwenye akaunti yake.Akaunti hii imeunganisha kwenye mtandao wetu wa BancABC Mobi kupitia USSD (15034#) na Aplikesheni yetu kwa hivyo mteja haitaji kila mara kutembelea matawi yetu kwa ajili ya kuweka au kutoa hela. Vile vile mteja anaweza kutumia akaunti yake kupitia machine za ATM zenye nembo ya Visa, mawakala wa BancABC pamoja na “internet banking” Mteja wa IZZE akaunti atapata huduma hizi zote za kibenki kwa masaa 24 siku saba za wiki popote alipo. Zaidi, mteja atakuwa akipata ujumbe mfupi kupitia simu ya kikanjani yaani sms kila mara anapofanya muamala wa kuweka ama kutoa pesa bure na kupata huduma ya mikopo baada ya hapo.Kwa upande wake, Meneja wa huduma za uwakala wa benki hiyo Ndugu, Mwita Rhobi alisema kuwa BancABC imewawezesha mawakala ambao wanapatikana nchini kote kusaidia zoezi la ufunguaji wa akaunti ya IZZE. Mawakala hawa wataweza kufanya hatua zote za kufungua akaunti kidigitali na mtu yeyote anayehitaji kufungua akaunti ya IZZE atafanikisha huduma hiyo kwa muda usiozidi dakika tano. | 5 |
Uwepo wa Salum Telela, Patto Ngonyani na Thabani Kamusoko, kumemfanya kocha Hans Pluijm, kumuweka benchi kiungo huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi nyingi za ulinzi.Akizungumza na gazeti hili, Twite alisema hajajua kama msimu ujao atasalimika na janga la kutemwa kutokana na nafasi ndogo anayoipata ya kucheza kwenye mechi za timu hiyo tangu kuanza msimu huu, licha ya kucheza kwa kujituma mazoezini.“Msimu huu umekuwa na changamoto, kubwa ni kuwania nafasi ya kucheza na wachezaji vijana, mechi nyingi nimekuwa nikianzia benchi, kitu ambacho kinanipa hofu kwamba huenda nikaoneshwa mlango wa kutokea ukizingatia mkataba wangu unamalizika baada ya ligi kuisha,” alisema.Twite, mzaliwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), alisema anajua kuwa kocha wake amepoteza imani na yeye kutokana na uwepo wa wachezaji hao anaocheza nao kwenye nafasi moja, lakini amekuwa akijitahidi kujituma mazoezini ili kumshawishi aweze kumtumia kikosi cha kwanza.Kiraka huyo aliyetamba na timu za APR ya Rwanda na FC Lupopo ya Congo, ametua Yanga misimu minne iliyopita, na ameichezea kwa mafanikio timu hiyo na kufanikiwa kuipa mataji mawili ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara. | 4 |
NA CHRISTOPHER MSEKENA
UNAWEZA kumpeleka ng’ombe mtoni kwa kutumia nguvu nyingi, ila ukashindwa kutumia nguvu hiyo hiyo kumfanya anywe maji ya mto, kwa kuwa uamuzi wa kunywa au kutokunywa ni wake.
Mapema wiki hii jijini Dar es Salaam baadhi ya wasanii wa filamu walifanya maandamano ya kupinga uuzwaji wa filamu za nje zisizofuata utaratibu kwa kile walichodai zinashusha soko la filamu za ndani.
Hapo ndipo gumzo lilipoanzia. Kuna kundi kubwa la watu waliounga mkono tukio hilo na wengine wengi, wakiwamo mastaa walipinga kitendo hicho.
Ninachokiona
Kuna ufa mkubwa kwenye tasnia ya filamu na endapo usipozibwa tutashuhudia tasnia hii ikikosa mwelekeo na kupoteza ajira za vijana wengi wanaotegemea sanaa kuendesha maisha yao.
Umoja wa wasanii umebaki kwenye vyama pekee na siyo ndani ya mioyo ya wanachama, yaani wasanii. Iweje wasanii waliopo kwenye chama kimoja wagawanyike kwenye hili lililobeba taswira ya kuijenga sanaa.
Iweje JB, Ray, Richie Richie, Wolper, Kajala na wengine waandamane na punde aibuke Steve Nyerere na kupinga kwa hoja walichokifanya wenzake.
Tujikumbushe hii
Kipindi cha nyuma kabla hatujaanza kutengeneza filamu zetu, tulikuwa tukipata uhondo wa filamu za Marekani, Uingireza, China, India na kwingineko.
Hakika tulifaidi utamu wa sanaa ya kina Arnold Schwarzenegger, Rambo, Jet Li, Donnie Yen, Bruce Lee, Steven Seagal, Amitabh Bachchan, Sunny Deol na wengine wengi kwenye vibanda umiza kule mtaani.
Baadaye zikaja filamu za Nigeria ambazo zilipoteza umaarufu wake Tanzania ilipoanza kutengeneza michezo ya kuigiza katika runinga (Tamthilia) na hatimaye zikazaliwa filamu zilizofanya vizuri sokoni na kutuletea mastaa hawa tunaowaona.
Unaweza kuona ni namna gani filamu kutoka nje zilivyoamsha akili zetu na sisi tukathubutu kuingia kwenye utengenezaji na kufanikiwa kutamba mpaka nje ya mipaka yetu, sasa iweje leo tuseme filamu kutoka nje zinaua soko la ndani.
Kilichoikumba tasnia
Baada ya kupata ustaa na kujizolea mashabiki wengi, wasanii wetu wamekuwa wakifanya kazi zao kwa mazoea, wakijua kabisa ni lazima mashabiki watanunua siyo kwa kupenda maudhui ya kazi, bali kwa ajili ya ukubwa wa majina yao.
Mfano mdogo ni huu, hebu linganisha kava za filamu zetu na zile za nje, utaona filamu zetu zikipambwa na mastaa wakubwa na warembo wenye maumbo ya kuvutia wakati wenzetu hawategemei hayo kuuza filamu zao.
Weledi wa kazi umepungua, filamu zetu hazina ubora unaokidhi, hakuna uwekezaji unaofanyika, hakuna mawazo mapya kwenye tasnia, ndiyo maana lokesheni kila siku ni zile zile kiasi kwamba mashabiki wamechoka na kuamua kutazama filamu za Kikorea zenye ladha waliyoikosa nyumbani.
Ukweli filamu za nje
Siungi mkono uuzwaji usio halali wa CD zenye maudhui ya picha jongevu kutoka nje kwa sababu serikali inapoteza mapato. Kinachofanyika ni kwamba, mtu anapakua filamu ya nje kwenye mtandao, anaiweka kwenye CD, anatengeneza kava zuri na kuiingiza mtaani kwa bei isiyozidi elfu 2 na ndani yake zitapatikana nyongeza ya filamu zaidi ya tano.
Kwa kuwa maudhui yanavutia, shabiki anaacha kununua filamu ya kibongo inayouzwa elfu 5 yenye maudhui aliyoyazoea na kununua ya Adaan, filamu itakayokata kiu yake kwa bei rahisi.
Wasanii fanyeni haya machache
Kwanza kuweni wamoja ili mpiganie na mpate sheria mpya ya filamu itakayowalinda nyinyi na kazi zenu, pili jiulizeni kitu gani kimekosekana kwenye filamu zenu mpaka mapenzi ya mashabiki yamehamia ughaibuni.
Mkifanikisha hayo, hamtakuwa na haja ya kuandamana wala kumuona Mkorea kama nuksi kwenu, kumbukeni mashabiki wanataka ladha mpya, fanyeni kazi na muache kuchezea sanaa yenu, nadhani nimeeleweka. | 1 |
Na LEONARD MANG’OHA -DAR ES SALAAM Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Amiri Manento, amesema haki ya kupata taarifa ni kiashiria kimojawapo cha serikali yenye uwazi ambayo inathamini mchango na ushiriki wa wananchi katika ujenzi wa taifa. Alikuwa akizungumza Dar es Salaam jana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya upatikanaji wa taarifa. Jaji Manento alisema haki hiyo ni ya kila mtu hivyo inapaswa kulindwa kwa nguvu zote. “Lengo la maadhimisho haya ni kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya haki ya kila mtu kupata taarifa muhimu kwa maisha yao, zilizopo katika hifadhi ya serikali na kwingineko. “Haki ya kufahamu namna viongozi waliowachagua wanavyotekeleza majukumu yao na namna fedha za walipa kodi zinavyotumika,” alisema Jaji Manento. Alisema haki hiyo ya kupata taarifa ni mojawapo ya nguzo kuu ya tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu la mwaka 1948 ambalo Tanzania pia ni mwanachama. Alisema Tanzania iliridhia azimio la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu baada ya kupata uhuru pamoja na mkataba wa haki za raia na siasa hivyo inawajibika kuutekeleza. “Haki ya kupata taarifa na wajibu wa kutoa habari unaimarisha misingi ya utawala bora ikiwamo uwazi, ushirikishwaji, uwajibikaji na utawala wa sheria. “Watendaji wa Serikali watafanya kazi zao kwa uwazi na wananchi kwa ujumla wao hata mmoja mmoja watashiriki na watendaji hao watawajibika kwa wananchi wao katika kila ngazi ya utendaji na hatimaye utawala bora utaimarika,”alisema Jaji Manento. Aliitaka Serikali kuhakikisha inatunga kanuni na sheria ya haki ya kupata taarifa ya 2016 kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wananchi. Jaji Manento aliwataka wadau wa habari wakiwamo waandishi wa habari na taasisi zisizo za kiserikali kuendelea kupaza sauti kudai haki ya kupata taarifa kwa sababu watoa taarifa hizo wanaweza kujisahau. Akizungumza katika maadhimisho hayo, mwandishi mkongwe ambaye pia ni mwanasheria, Jenerali Ulimwengu, alisema kucheleweshwa kutungwa kanuni za sheria ya haki ya kupata habari iliyotungwa mwaka jana na kuidhinishwa na Rais kumesababishwa asasi za raia na vyombo vya habari kuendelea kufungiwa. “Tunapojadili suala hili tuangalie uwezo tuliokuwa nao au tuliotarajiwa kuwa nao, je tunao au umeminywa kabisa? “Tangu sheria hii ipitishwe haijachapishwa katika gazeti la serikali wala kutungiwa kanuni na tumeona magazeti yakifungiwa. “Uhuru wa kujieleza ndiyo mama wa uhuru wote, kama huna uhuru wa kusema nina njaa, uhuru wa kupata chakula, utatoka wapi?” alihoji. Naye Mkurugenzi wa Sikika, Irenei Sungura, alisema ukimnyima mtu nafasi ya kujieleza unampa nafasi ya kufikiria zaidi hata yale ambayo asingeweza kuyafikiria kama angepewa uhuru. “Sasa unapolifungia gazeti ambalo limechapisha taarifa ambayo ilikuwa imeenea kwenye mitandao, je unapozuia mtoa taarifa sisi wananchi tunaopokea taarifa hizo tuajua kuzichakata kujua ipi sahihi?” alihoji. Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda alisema mapambano dhidi ya sheria kandamizi kwa vyombo vya habari hayajaanza leo, kwa sababu yamekuwapo kwa muda mrefu. “Tatizo tunaongozwa na chama kile kile na watu wale wale na wenye mitazamo ile ile, hata akizaliwa Waziri Mkuu mpya, Makamu wa Rais Mpya japo atakuja na staili mpya ataendeleza yale yale. “Kwa sababu ilianza wakati wa Mkapa (Benjamin) alipoandikwa akiwa kule Tabora aliwatisha wamiliki wa vyombo vya habari kuwa wataeleza wanakotoa mitaji, akaja aliyefuata Kikwete akajionuesha ana urafiki na vyombo vya habari kwa kutaka kuonekana,” alisema Kibanda. Alisema kwa sasa Tanzania imekuwa na idadi kubwa ya watu wajinga kuliko ilivyokuwa zamani kutokana na kuminywa kwa uhuru wa kupata taarifa ikiwamo Bunge kutooneshwa mubashara (live) na kuchaguliwa baadhi tu ya matukio ya kuonyeshwa. Kuhusu mashambulio mbalimbali likiwamo la hivi karibuni dhidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, alisema si geni bali ni mwendelezo wa matukio hayo tangu awamu zilizopita. Mwakilishi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Anna Henga, alisema kwa sasa haki hiyo imeshuka sana na jamii wakiwamo waandishi wa habari wamejawa woga wa kuhoji mambo mbalimbali yanayohusu jamii. | 3 |
DHAMIRA ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuinua uchumi kupitia sekta ya viwanda, inazidi kupata nguvu na kuungwa mkono na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.Mwekezaji mzawa ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group, Mohammed Kiluwa ametangaza dhamira ya kuwekeza katika miundombinu ya usafirishaji kwa kujenga kiwanda cha mabehewa kwa ajili ya reli za kisasa na za zamani.Akiwa katika hafla ya kubadilishana nyaraka za makubaliano hayo aliyoingia na Kampuni ya Africa Jambo Group ya Afrika Kusini jijini Johannesburg hivi karibuni, Kiluwa amesema anataka kufanya kitu cha kipekee katika ardhi ya Tanzania kwa faida ya nchi na mataifa mengine barani Afrika.“Hiki tunachotaka kukifanya hakijawahi kufikiriwa na wengi, lakini kitaleta tija katika uchumi wa nchi. Tunafahamu tunapoelekea ni Tanzania ya viwanda na uchumi wa kati. Tutahitaji mbinu bora za usafirishaji malighafi na bidhaa, reli ni njia rahisi na salama kusafirishia mizigo,” amesema Kiluwa.Amebainisha kuwa, kiwanda hicho kitajengwa katika eneo la uwekezaji Kiluwa Free Processing Zone mkoani Pwani na kitagharimu Dola za Marekani milioni 150 (karibu Sh bilioni 360). Utekelezaji wa mradi huo unaolenga soko la ndani la Tanzania na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Afrika kwa ujumla, unatarajiwa kufanyika katika awamu tatu huku kila awamu ikiajiri watu 980.Alisisitiza kuwa, wakazi wa nchi za EAC watakuwa sehemu ya wanufaika kwa kuwa baadhi ya mizigo itakayosafirishwa katika mabehewa hayo itakwenda katika nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi hadi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na nyingine za ukanda wa kusini mwa Afrika.“Ifahamike tumetenga kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 150, kwa ajili ya kukamilisha mradi huu ambao utaleta mapinduzi makubwa katika sekta ya viwanda nchini pamoja na usafirishaji,” amesema Kiluwa.Mwakilishi wa Kampuni ya Africa Jambo Group, Marthinus Christian Landman alisema wameamua kuwekeza Tanzania kwa sababu wanajua ni eneo muhimu linalokua kwa kasi kiuchumi kutokana na malengo makubwa yaliyowekwa na serikali iliyopo madarakani.“Siku zote mfanyabiashara anaangalia eneo ambalo atanufaika, tunaangalia zaidi faida kabla ya kukamilisha mikataba, tumejiridhisha kwa sasa Tanzania ni sehemu sahihi na salama kiuwekezaji kwa sababu Rais John Magufuli amedhamiria kuona watu wanafanya kazi, hakuna kona kona wala rushwa,” alisema Landman.Tangu Rais Magufuli aingie madarakani Novemba 5, mwaka 2015, alikuja na falsafa ya kuijenga nchi kupitia uchumi wa viwanda ili hatimaye nchi iingie kwa kasi katika uchumi wa kati.Mwito huo umeitikiwa kwa kasi kubwa kutokana na wawekezaji wa ndani na nje kutokana na kujenga viwanda vya kila aina katika kila pande za nchi, hali inayoleta matumaini mapya kwamba muda si mrefu ndoto za Rais Magufuli za `Mapinduzi ya Viwanda’ zitatimia. | 3 |
Mwandishi wetu, Tanga MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema kampeni ya elimu kwa mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) itawasaidia wafanyabiashara wanaokwepa kodi kuacha vitendo hivyo vya kuikosesha Serikali mapato. Shigela ameyasema hayo ofisini kwake alipotembelewa na maafisa wa TRAwanaofanya kampeni hiyo mkoani humo ambayo imelenga kuwaelimishawafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati. Amesema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi pengine kwa kujua au kutokua, jambo ambalo linahitaji elimu ya uelewa ili kila mwananchi afahamu wajibu wake kwenye ulipaji wa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Akiizungumzia kampeni hiyo, Shigela ameipongeza TRA kwa kuendesha zoezi hilo katika mikoa mbalimbali na kusema litaongeza ukusanyaji wa mapato baada ya wafanyabiashara kuelimishwa na kufahamu kuwa maendeleo ya nchi yanasababishwa na ulipaji wa kodi kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, barabara, umeme na maji. Shigela amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanalipa kodi kwa hiari bila kusubiri kubugudhiwa na serikali, huku akieleza kuwa serikali itaendelea kupambana na wakwepa kodi wanaoingiza bidhaa za magendo nchini kwa kupitia bandari bubu zilizopo kandokando ya Bahari ya Hindi. “Nchi yoyote haiwezi kupiga hatua ya maendeleo bila wananchi wake kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa sababu kodi ndio kila kitu huwezi kujenga barabara kama wafanyabiashara hawataki kulipa kodi, huwezi kuimarisha huduma za afya kama hakuna kodi na pia huwezi kuimarisha mifumo ya elimu bila kodi,” alisema Shigela. Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Tanga, Specioza Owure amesema kuwa, maafisa hao wa TRA wanaofanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi, watafika maeneo mbalimbali yenye wafanyabiashara katika mkoa wa Tanga na watawaelimisha kuhusu umuhimu wa kodi na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. “Maafisa hawa wanatumia jitihada zote kuwaelimisha wafanyabiashara, tunafanya hivi ili kila mmoja afahamu wajibu wake wa kulipa kodi sambamba na kusogeza huduma za TRA karibu na wateja,” alisema Owure.Kampeni ya elimu kwa mlipakodi mkoani Tanga inatarajia kumalizika Juni 30, 2020 ambapo lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara, kusikiliza maoni na changamoto zao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. | 5 |
['Inter Milan wako tayari kulipa £11m na ada zingine ili kumsajili kiungo wa kati Christian Eriksen kutoka Tottenham mwezi huu. (Sky Sports)', 'Manchester United inaandaa ofa ya £43m kumnunua mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Moussa Dembele, baada ya Marcus Rashford kuumia mgongo. (Foot Mercato, via Manchester Evening News)', 'Manchester United watalazimika kulipa ada ya juu ya uhamisho kumpata mshambuliaji wa Paris St-Germain na Uruguay Edinson Cavani, 32, mwezi huu badala ya kumchukua kwa mkopo - lakini mchezaji huyo yuko tayari kuondoka PSG. (Manchester Evening News)', 'Kujiunga na Liverpool ndio "lengo kuu" la mshambuliaji wa RB Leipzig na Ujerumani Timo Werner, 23, ambaye anataka kucheza katika ligi kuu ya premia. (Bild, via Sport Witness)', 'Inter Milan wanakaribia kumsajili kwa mkopo beki wa Chelsea Victor Moses, 29, kujiunga na mkufunzi wake wa zamani Antonio Conte. Fenerbahce, klabu ambayo kiungo huyo wa kimataifa wa Nigeria anachezea kwa mkopo imeridhia kumuachilia. (Mail)', 'Mkufunzi wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger anasema Gunners "ilituvunja moyo" lipoondoka Highbury na kuhamia uwanja wa Emirates. (Evening Standard)', 'Everton imekataa ofa mbili za kumnunua beki Mason Holgate, huku Newcastle, Bournemouth na Sheffield United zikiwa miongoni mwa timu zinazomtaka mchezaji huyo wa miaka 23. (Football Insider)', 'Liverpool haiko tayari kumpoteza kiungo wa kati wa Uswizi Xherdan Shaqiri, 28, licha ya Roma kuonesha nia ya kutaka kumnunua mwezi huu. (Sky Sports)', "Manchester United imekiri kuwa ilishindwa na Real Madrid katika kinyang'anyiro cha usajili wa kiungo wa kati wa Ajax Donny van de Beek, 22. (Star)", 'Klabu ya Uhispania ya Celta Vigo imekuwa ikiwasiliana na Southampton kuhusu uhamisho wa kiungo wa kati, Oriol Romeu lakini Saints hawataki Mhispania huyo wa miaka 28-kuondoka (Southern Daily Echo)', 'Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal na Manchester United Robin van Persie ameionya United kutokimbilia kumrudisha uwanjani Marcus Rashford, 22, baaada ya kiungo huyo mshambulizi kuumia mgongo. (Manchester Evening News)', 'Bournemouth wanamtaka winga wa Borussia Dortmund Jacob Bruun Larsen, 21, lakini mkufunzi wa Cherries Eddie Howe amesema hakuna mchezaji mpya atakayejiunga nao. (Daily Echo)'] | 4 |
NA BADI MCHOMOLO ZIMEBAKI siku 12 kuelekea kwenye kivumbi cha michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi Juni 14. Jumla ya miji 11 itatumika kwa ajili ya michuano hiyo ambayo itafanyika kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi Julai 15. Timu 32 kutoka mataifa mbalimbali zinaendelea kufanya maandalizi ya vikosi vyao ili kuona uwezekano wa kuandika historia kwa kutwaa taji hilo. Ubora wa wachezaji pamoja na mifumo ya makocha ndiyo chachu ya mafanikio ya timu kutwaa taji hilo, hivyo kila kocha ametaja kikosi chake chenye wachezaji ambao wamekamilika kuanzia safu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji. Timu ambayo itakuwa na ubora katika safu ya ushambuliaji na ulinzi inaweza kufanya vizuri na kuandika historia, wafuatao ni baadhi ya mabeki wanaotajwa kuwa katili na wakuchungwa kwenye michuano hiyo. Sergio Ramos (Hispania) Ana umri wa miaka 32, ni miongoni mwa wachezaji wenye uwezo mkubwa na msaada kwa timu yao hasa katika safu ya ulinzi, amekuwa na uzoefu wa michuano hiyo mikubwa. Atakuwa anakiongoza kikosi cha timu ya taifa ya Hispania katika safu ya ulinzi, anatajwa kuwa miongoni mwa mabeki katili kwa kipindi hiki. Mei 26, mchezaji huyo wa klabu ya Real Madrid, alilifanya jina lake lisikauke kwenye midomo ya watu baada ya kumchezea vibaya mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah. Zaidi ya mashabiki 500,000 walisaini pendekezo la kuwaomba Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) na Chama cha Soka Ulaya (UEFA), achukuliwe hatua kutokana na kitendo chake, hivyo ni mmoja kati ya mabeki wa kuchungwa huko Urusi kwenye Kombe la Dunia. Thiago Silva (Brazil) Ni beki wa kati wa klabu ya PSG pamoja na timu ya taifa ya Brazil, amekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya klabu hiyo pamoja na timu ya taifa. Anatajwa kuwa miongoni mwa mabeki wenye akili nyingi wakiwa uwanjani kwa kucheza mpira kwa umakini wa hali ya juu. Mbali na upole wa mchezaji huyo, lakini anatajwa kuwa miongoni mwa mabeki katili. Pepe (Ureno) Miongoni mwa mabeki ambao walikuwa na mchango mkubwa katika klabu ya Real Madrid misimu iliyopita ni pamoja na Kepler de Lima maarufu kwa jina la Pepe. Kwa sasa mchezaji huyo anakipiga katika klabu ya Besiktas baada ya kuondoka Madrid, mchezaji huyo yupo kwenye kikosi cha Ureno kuelekea Kombe la Dunia nchini Urusi. Pepe ni mmoja kati ya mabeki wenye roho mbaya na amekuwa akioneshwa kadi za njano na nyekundu mara kwa mara kutokana na ukatili wake. Vladimir Granat (Urusi) Wenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia timu ya taifa ya Urusi wanaamini safu yao ya ulinzi ipo sehemu salama kutokana na ubora wa beki wao wa kati, Granat. Beki huyo anakipiga katika klabu ya Rubin Kazan, inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo, amekuwa akihakikisha ulinzi kwa timu yake kwa kuwafanya washambuliaji wasipate nafasi ya kupita. Nicolas Otamendi (Argentina) Amekuwa na mchango mkubwa katika klabu ya Manchester City msimu huu, ameweza kuwadhibiti wapinzani na kuifanya timu hiyo ichukue ubingwa wa Ligi Kuu England. Kikosi cha timu ya taifa ya Argentina kimempa mchezaji huyo jukumu la kulibeba taifa kwenye michuano ya Kombe la Dunia kwa kuweka ulinzi imara kama alivyofanya ndani ya Man City. Diego Godin (Uruguay) Katika kikosi cha Atletico Madrid, mchezaji huyo amekuwa akisimama vizuri kwenye nafasi yake ya ulinzi hadi timu hiyo inamaliza nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi nchini Hispania. Kutokana na ubora wake na umakini katika safu ya ushambuliaji, mchezaji huyo atakiongoza kikosi cha Uruguay kwa kuweka ulinzi kwa mlinda mlango wake. Samuel Umtiti (Ufaransa) Mchezaji huyo alimfanya beki wa kati wa Barcelona, Gerard Pique, kuwa na wakati wa kupumzika kutokana na ubora wake. Mara nyingi alionekana kupambana na washambuliaji kwenye michuano ya Ligi Kuu nchini Hispania na kufanikiwa kutwaa ubingwa, alikuwa anaonekana kuwa na roho mbaya uwanjani hasa kutokana na rangi yake nyeusi, hivyo Ufaransa wanaamini wapo sehemu salama kwa uwepo wa mchezaji huyo. Cristian Zapata (Colombia) Klabu ya AC Milan iliwahi kuwa na beki mwenye roho mbaya miaka ya nyuma akijulikana kwa jina la Gennaro Gattuso, lakini kwa sasa yeye ni kocha wa timu hiyo. Beki ambayo anatajwa kuchukua baadhi za tabia za mchezaji huyo ni Cristian Zapata raia wa nchini Colombia, hivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, amepewa jukumu la kuwazuia washambuliaji ambao watakuwa na nia ya kuwafunga kwenye michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi. Raphael Varane (Ufaransa) Mwonekano wake akiwa uwanjani ni kama mpole sana huku miguu yake ikiwa na matege, lakini amekuwa akiimarisha ulinzi katika kikosi cha Real Madrid pamoja na timu ya taifa ya Ufaransa, amekuwa akipambana na washambuliaji wenye kasi kwa kuwachezea vibaya, hivyo atakuwepo kwenye Kombe la Dunia nchini Urusi. Hao ni baadhi ya mabeki wa kuangaliwa kwenye Kombe la Dunia mwaka huu | 4 |
MANCHESTER, ENGLAND KOCHA mpya wa klabu ya Crystal Palace, Roy Hodgson, amesema ubora wa klabu ya Manchester United ni sawa na bondia mwenye uwezo wa hali ya juu. Manchester United juzi ilishuka dimbani kwenye Uwanja wa nyumbani wa Old Trafford na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Crystal Palace, hivyo Hodgson amedai hawakuwa na uwezo wa kuwazuia wapinzani hao wasiibuke na ushindi. Mchezo huo ulikuwa wa saba katika michuano hiyo ya ligi kuu msimu huu, lakini Crystal Palace haikufanikiwa kupata ushindi kwa michezo yote na kuifanya ishike nafasi ya mwisho kwenye msimamo. Hodgson mwenye umri wa miaka 70, amekuwa kwenye kazi ya ukocha kwa miaka 40 huku akifundisha jumla ya timu 21 tofuti, alichukua nafasi ya kuifundisha klabu hiyo ya Crystal Palace baada ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Franke de Boer, kufukuzwa kazi kutokana na kupoteza michezo mitano ya ligi, hivyo Hudgson amekiri kuwa Man United ni habari nyingine. “Nadhani lazima tukubaliane na matokeo, tulikutana na klabu ambayo ilikuwa kwenye uwezo wa hali ya juu kama bondia, hivyo tulikuwa na kila sababu ya kufungwa katika mchezo huo, siwezi kuwalalamikia wachezaji kwa kuwa hawakuwa na jinsi walizidiwa kila idara. “Kikubwa ni kujipanga kwa ajili ya michezo inayofuata, ninaamini nitapambana kuhakikisha tunaleta furaha kwa mashabiki na kuondoka kwenye nafasi tuliopo kwa sasa,” alisema Hodgson. Hata hivyo, kocha huyo anaamini kuwa kikosi chake kisingefungwa mabao mengi endapo wachezaji wake nane majeruhi wangekuwepo kama vile Christian Benteke, Wilfried Zaha, Ruben Loftus-Cheek na wengine. Mchezo unaofuata Crystal Palace watakuwa kwenye Uwanja wa nyumbani Oktoba 14 dhidi ya mabingwa watetezi, huo utakuwa mtihani mwingine kwa kocha Hodgson ambaye ana kazi ngumu kuhakikisha timu hiyo inabaki kwenye ligi msimu ujao.
| 4 |
Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM
KATI ya Novemba 25 hadi Desemba mosi, 2017 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), ilifanya upasuaji mkubwa wa moyo wa kihistoria nchini.
Madaktari Bingwa wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Open Heart International kutoka nchini Austraria waliwafanyia upasuaji wagonjwa 16 wenye matatizo mbalimbali ya moyo.
Kati ya wagonjwa hao, tisa walikuwa watoto na saba watu wazima, ambao walifanyiwa upasuaji wa kubadilisha milango ya moyo iliyokuwa imeharibika na kuwekewa milango ya chuma.
Miongoni mwa watu wazima waliofanyiwa upasuaji wapo waliopandikizwa mishipa ya damu iliyovunwa kutoka miguuni na kwenda kuzibua ile iliyokuwa imeziba.
“Upasuaji huo kitaalamu unaitwa ‘bi-pass surger,’ hii si mara ya kwanza kwa taasisi yetu kufanya kwani tayari wagonjwa wapatao 30 wamefanyiwa kwa mwaka huu pekee,” anasema Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi.
Anasema: “Watoto waliofanyiwa upasuaji walikuwa na umri wa kuanzia miezi minne wakiwa na uzito wa kuanzia kilo nne hadi 12, kati yao, mmoja alikuwa amezaliwa akiwa na moyo upande wa kulia.”
Profesa Janabi anasema kibaiolojia moyo wa binadamu unapaswa kuwa upande wa kushoto hata hivyo, hutokea mara chache mtoto kuzaliwa moyo ukiwa upande wa kulia.
Anasema hadi sasa bado haijajulikana wazi nini hasa husababisha mtoto kuzaliwa moyo ukiwa upande wa kulia.
“Duniani, tafiti zinaonesha kati ya watoto 2000 wanaozaliwa basi mmoja huwa katika uwezekano wa kuzaliwa moyo wake ukiwa upande wa kulia,” anasema.
Anasema hata hivyo hakuna madhara yoyote yanayoweza kumpata mtoto ambaye moyo wake umeumbwa ukiwa upande wa kulia.
“Anaweza kuishi vema kabisa kama binadamu wengine ambao wameumbwa wakiwa na moyo katika upande wa kushoto,” anabainisha. Mtoto aliyefanyiwa upasuaji
Profesa Janabi anasema mtoto ambaye walilazimika kumfanyia upasuaji alikuwa na matatizo makubwa mawili ya moyo.
“Moyo kuumbwa upande wa kulia haikuwa tatizo kubwa kwake, isipokuwa tulibaini mishipa yake ya damu ilikuwa haifanyi kazi inavyopaswa.
“Katika moyo kuna mishipa inayoingia upande wa kulia ambayo kazi yake kuu ni kubeba damu chafu yenye hewa ya kabondaioksaidi na kuna inayoingia upande wa kushoto yenyewe hubeba damu safi yenye oksijeni,” anabainisha.
Anaongeza: “Huyu mishipa yake ilikuwa inachanganya damu safi na chafu kwa pamoja jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwa maisha yake.
“Ni kama vile uchukue maji safi na taka halafu uyachanganye kwa pamoja kisha unywe, kamwe mwili hauwezi kuhimili mchanganyiko huo.
“Sasa yeye badala ya damu chafu kupita katika upande unaostahili ili ikasafishwe huchanganyika pamoja na damu safi iliyokwisha safishwa kisha iende mwilini kutumika, ni tatizo,” anasema.
Anasema pamoja na tatizo hilo, tatizo jingine lilikuwa ni mapigo yake ya moyo yalikuwa chini mno kutokana na kiwango kidogo cha umeme kilichopo kwenye moyo wake.
“Kutokana na hali hiyo, ilibidi tumpandikize betri ndani ya moyo wake, hii ni oparesheni ya tatu kwa watoto na sasa mapigo yake yanakwenda vema,” anasema.
Anasema ilichukua takriban saa tisa kukamilisha upasuaji huo kwa sababu kwa kesi kubwa kama hiyo huwalazimu ‘kuusimamisha’ moyo wake kwa saa kadhaa. Mwili kuwa na rangi ya bluu
Anasema damu safi na chafu inapochanganyika ni lazima mwili wa mgonjwa ubadilike rangi na kuwa bluu.
“Kitendo cha kubadilika na kuwa rangi ya bluu maana yake ni kwamba kile kiwango cha oksjeni kinachohitajika mwilini huwa hakitoshelezi,” anabainisha. Dalili zake
Anataja dalili za awali kwa mtoto aliyezaliwa na tatizo la moyo ambazo mzazi anaweza kuziona ni pamoja na kushindwa kunyonya vizuri.
Anasema hii huwatokea zaidi watoto walio katika umri wa kunyonya, lakini kwa wenye umri wa kwenda shule wengi huchoka mara kwa mara. Makuzi baada ya upasuaji
Anasema mtoto waliyemfanyia upasuaji ataendeelea vizuri na kwamba ataishi na kulelewa kama ilivyo kwa watoto wengine wasio na tatizo.
“Kila mshipa wa damu sasa unafanya kazi yake kama inavyotakiwa na mfumo wa umeme upo sawa sawa baada ya kumpandikiza betri.
“Lakini kama asingetibiwa mapema basi kidaktari naweza kusema wazi kwamba asingefika na kusherehekea sikukuu yake ya kuzaliwa ya mwaka mmoja.
“Ila kwa kuwa tumewahi kumfanyia upasuaji tunaamini Mungu akimjalia basi atasherehekea sikukuu yake ya mwaka wa kwanza na kuendelea,” anasema. Masharti
Anasema mtoto huyo ambaye ni mchanga, ataishi na kula kila kitu isipokuwa amepewa masharti kadhaa.
“Tumempatia kadi maalumu ya utambuzi, hatatakiwa kupita katika maeneo yenye sumaku kubwa kama vile uwanja wa ndege kwa sababu ile nguvu inaweza kukiwasha na kuyafanya mapigo ya moyo kubadilika na kwenda kasi,” anasema. Ushirikiano zaidi
Mkufunzi wa Wagonjwa Mahututi na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa OHI, Russel Lee anasema wataendelea kushirikiana kwa ukaribu na JKIC katika kutoa matibabu.
“Kila ninapokuja Tanzania naona JKCI inazidi kufanya matibabu kwa kiwango cha juu zaidi ya awali, hili ni jambo linalotia faraja kubwa, OHI tutaendelea kushirikiana nao pia kwa kuwapatia mafunzo wataalamu wake ili wazidi kufanya vizuri zaidi,” anasema.
Daktari Bingwa wa Upasuaji Magonjwa ya Moyo kwa Watoto wa JKCI, Godwin Sharau anasema faida kubwa wanayopata katika kambi hizo za matibabu ni kubadilishana ujuzi.
“Kuna baadhi ya magonjwa ya moyo ambayo ni magumu na JKCI tunahitaji kupanda hatua kwa hatua ili tuweze kuwahudumia vizuri watoto na wakubwa wenye matatizo haya.
“Tunataka twende sambamba na wenzetu katika teknolojia ya kutibu magonjwa ya moyo ili kufikia adhma ya serikali kupunguza idadi ya wagonjwa wanaoenda kutibiwa nje ya nchi,” anasema. Wito
Anawasihi wazazi wanapoona dalili hizo wawahi kuwapeleka watoto wao hospitalini kwa uchunguzi zaidi.
“Ukimpeleka hospitalini watabaini tatizo na kama anastahili kuletwa JKCI watampa rufaa kuja huku, kuendelea kukaa naye nyumbani kutahatarisha zaidi maisha yake hatimaye kifo.
Anasema katika kipindi cha mwaka huu pekee wamewafanyia upasuaji watoto 300 wenye matatizo ya moyo, ukijumlisha na watu wazima idadi yao inazidi 600.
“Watoto waliopoteza maisha ni wanne tu, hivyo wasiogope kuja kuwafanyia uchunguzi na upasuaji watoto wao,” anawasihi.
Profesa Janabi anawahimiza pia wataalamu wa afya kuhakikisha wanawapa rufaa mapema kwenda JKCI watoto wanaowapokea wakiwa na dalili za maradhi makubwa ya moyo. | 0 |
KLABU ya Yanga imesema ili kupata saini za wachezaji inaowahitaji na wanatumikia timu zao za taifa kwa ajili ya maandalizi ya fainali za Afrika (Afcon) watamtumia Kocha wao Mwinyi Zahera (pichani) kumaliza kazi.Timu hiyo imekuwa ikiendelea kujiimarisha katika usajili wa wachezaji wa kimataifa na ndani kwa maandalizi ya Ligi Kuu na michuano ya Afrika msimu ujao. Akizungumza na gazeti hili juzi Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela alisema wapo baadhi ya wachezaji wameshamalizana nao na kinachosubiriwa ni kupelekewa mikataba kwa njia ya mtandao ambapo Zahera atapokea kule na kumaliza kazi.Zahera atakuwepo Misri na kikosi chake cha timu ya taifa ya DR. Congo kama Kocha Msaidizi. “Kila mchezaji tunayemtaka hakuna litakaloshindikana Kocha atakuwepo kule tutawasiliana naye na kutuma mikataba kwa kutumia mtandao yeye atamalizia,”alisema.Klabu hiyo tayari imeshamalizana na wachezaji kadhaa wakiwemo beki Lamile Moro kutoka Ghana, mawinga Patrick Sibomana na Issa Bigirimana wote wa Rwanda, kiungo Abdulaziz Makame kutoka Mafunzo Zanzibar, Golikipa Metacha Mnata wa Mbao na mshambuliaji Sadney Urikhob kutoka Namibia. Pia, wako mbioni kunasa saini ya golikipa wa Kenya Farouk Shikalo na wachezaji wengine wanaotumikia timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars ambao bado hawajamalizana nao. | 4 |
Mwandishi Wetu -Katavi KAYA nne za Mtaa wa Rungwa Kata ya Kawajense, Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi zimeiomba serikali kuwasaidia fedha na mabati kwa ajili ya kujenga nyumba zao zilizobomolewa na mvua wiki moja iliyopita Wakizungumza jana waathirika hao walisema kuwa kwa sasa wanaishi kwa jamaa zao wakati wakijipanga kuanza ujenzi upya Mmoja wa waathirika wa tukio hilo, Agnes Pambe ni mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya Sekondari Rungwa alisema kuwa alikuwa na wadogo zake watatu wakati mvua inanyesha kisha ukuta wa chumba ukaanguka “Tulikimbilia nje mvua ikiendelea kunyesha na daadae nyumba yote ilianguka,” alisema Agnes Alisema anaishi na wadogo zake wanne; wawili kati yao wakiwa na umri wa chini ya miaka saba na kuongeza kuwa mama yao anafanya kazi ya kupika mgahawa katika kata ya machimboni na hivyo huja kuwasalimu kila akipata nafasi Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Rungwa, Felicia Mkota alisema alilazimika kuwatafutia watoto mahali pa kuishi kwa msamaria mwema, mpaka mama yao alipokuja baada ya siku tano na kuwapangishia chumba. | 0 |
Amina Omari -Tanga MKOA wa Tanga umesogeza huduma ya upimaji
wa ugonjwa wa dengue kutoka vituo vitatu hadi kufikia 11 kwa lengo la kuongeza
kasi ya upimaji ugonjwa huo. Hayo yamesemwa juzi na mratibu wa magonjwa
yanayopewa kipaumbele mkoani hapa, Josephine Kapinga wakati akitoa taarifa ya
udhibiti wa ugonjwa huo kwa waratibu wa afya na mazingira. Kapinga alisema kutokana na kuongezeka
vituo hivyo, kumesaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa ambao walikuwa
wanategemea vituo vichache. Alisema wizara husika imewasaidia vifaa
vya kupima bure ambavyo vimesambazwa vituo vya afya vya Serikali na kusababisha
kasi ya upimaji kuwa kubwa. “Kwa mfano, Julai hadi kufikia jana, kesi
za wagonjwa wa dengue zimepungua hadi kufikia mgonjwa mmoja pekee, inatokana na
elimu ya usafi inayoendelea kutolewa kwa wananchi,” alisema Kapinga. Alisema tangu Januari hadi Juni, mwaka
huu, wagonjwa waliopimwa ni 967, waliogundulika na ugonjwa huo ni 303, huku
kifo kikiwa ni kimoja, Wagonjwa wote walitoka Wilaya ya Tanga. Kapinga alisema tayari hatua mbalimbali za
kudhibiti ugonjwa huo zimeshachukuliwa, ikiwamo upuliziaji wa dawa katika
mabasi ya abiria, mifereji na makazi ya
watu. “Tayari Tanga Jiji wamefanikiwa kutoa
elimu ya kujikinga na ugonjwa huo kwa walimu 150 wa shule za msingi ili waweze
kutoa elimu,” alisema. | 0 |
WATOTO wenye umri wa kati ya miaka minne na 16 wanaoishi na kufanya kazi katika Mitaa ya Mji wa Sumbawanga mkoani Rukwa wamekuwa tishio kwa wakazi wa mji huo wakituhumiwa kwa uhalifu.Inadaiwa kuwa watoto hao wa kike na kiume katika umri huo mdogo ambao baadhi yao wameishi na kufanya kazi katika mitaa ya mji huo ambao ni makao makuu ya mkoa wa Rukwa kwa zaidi ya miaka 10, wamekuwa wakivunja nyumba 20 kila mwezi na kuiba mali na baadaye kuwajeruhi wenye nyumba.Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga , Dk Halfany Haule alisema hayo hivi karibuni mjini hapa wakati alipokaribishwa kutoa neno la utangulizi kama Mkuu wa Wilaya mwenyeji katika kikao kazi cha kujadili mpango mkakati na shirikishi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto wanaoishi humo Kikao hicho kiliratibiwa na kufadhiliwa na Plan International kupitia mradi wake wa Uzazi Salama Rukwa uliohudhuriwa na wataalamu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto mgeni rasmi akiwa Katibu Tawala wa mkoa, Benard Makali akimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Joachim Wangabo.“Kwa miaka 10 idadi ya watoto wanaoishi na kufanya kazi katika Mji wa Sumbawanga imekuwa ikiongezeka kwa kasi ya kutisha. Haya ni matokeo ya wazazi na walezi kuwafanyia ukatili watoto wao na kuwasababishia kukimbilia mjini Sumbawanga na kuishi katika mazingira magumu,” alisisitiza. Alikiri licha ya jitihada za mamlaka husika kukabili changamoto ya watoto hao, bado hazijazaa matunda.Akieleza sababu za watoto hao kuishi mitaani, Dk Haule alisema kwa familia za wakulima, ukifika msimu wa kilimo cha mahindi ambacho huchukua miezi sita wazazi na walezi wanahamia mashambani huku watoto wao wakibakia nyumbani na kuwaachia debe la unga na kilo kati ya tatu na tano za maharage. “Watoto hao wakipata nafasi ya kuishi mitaani na kuosha vyombo kwa mama ntilie huku ujira wao ukiwa chai ya asubuhi na milo ya uhakika ya mchana na usiku hawawezi kurejea kwao,” alisema Dk Haule.Makali alieleza katika kipindi cha Januari hadi Septemba, 2018, visa 1,234 vya ukatili dhidi ya watoto na 3,437 dhidi ya wanawake vimeripotiwa kwenye vituo vya polisi mkoani humo kwa hatua mbalimbali. Wakichangia baadhi ya wadau wamekiri changamoto kubwa ya watoto wanaoishi na kufanya kazi katika mitaa ya Sumbawanga inasababishwa na wazazi na walezi wao kuwatelekeza kwa kutowatimizia mahitaji.Machifu wa Kabila la Kifipa waliwataka wazazi na walezi wanaowatekeleza watoto wao waadhibiwe kimila ikiwemo kulipa mbuzi na kutengwa na jamii ili kusaidia kukomesha tatizo hilo mkoani humo. | 3 |
Je wewe ni right hand? Kama ni right hand najua kabisa kidole cha kwanza na cha pili baada ya kidole gumba ndo vinaweza kuwa vinafanya kazi kubwa sana kwenye mkono wako! Kwa vidole hivi kwangu mimi naweza kutype hii stori, Kutumia simu na hata kazi zingine, ha ha ha! Sasa bana asubuhi asubuhi mtandao kidogo umechafuka baada ya mwanadada na former Miss Tanzania wa mwaka 2006 Wema Sepetu kupost kaclip fulani ka video kwa IG yake vikionekana vidole vyake na hivyo vidole viwili havina kucha ndefu wakati vingine vinavyo. Acha sasa wananchi walivyoingia kwa kasi kukoment huku wakiuuliza kucha za hivyo vidole viwili amepeleka wapi. Wengine wameenda bali wakihusisha na matukio na tetesi za hivi karibuni za mlibwende huyo kudaiwa kuwa na urafiki ulio na mashaka na Diana Kimari ambaye ilidaiwa alipewa kichapo na Mama wa muigizaji huyo ili aachane na mwanae. VIDOLE vs DIANA = ? Umepata jibu ha aha ah! Wema mwenyewe baada ya kuona mambo yatakua makubwa alijiwahi kwenye caption na kuweka ujumbe unaonekana kutoa majibu juu ya zilipo kucha zake za vidole viwili. Wema aliandika; Oh He Looks sooo much like Daddy Sepetu… 😔😔😔 my big brother @amanisepetu
.
Colour collaboration on fleek… .
.
Kucha mbili sina… Msianze…!!! Caption hiyo bana haikuzuia wananchi kutoa dukuduku lao la moyoni na huku wengine wakidai hata hawakuona kama hana kucha Watu wanataka kucha bana! Si wakaendelea kuhoji; Wengine wakaachana na vidole wakaanza kuhoji juu ya kuwa kwake model! Hebu ngoja nisikuache hivi hivi hapa! Unadhani hivyo vidole viwili vinakazi gani? Maana koment zote hazijatoa jibu, karibu utiririke kwenye uwanja wa maoni; Oh He Looks sooo much like Daddy Sepetu… 😔😔😔 my big brother @amanisepetu . Colour collaboration on fleek… . . Kucha mbili sina… Msianze…!!! A post shared by Wema App (@wemasepetu) on Feb 4, 2020 at 7:27pm PST | 1 |
MWANDISHI WETU -TABORA MKUU wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, amesimamisha kwa muda likizo za watumishi wakiwemo wa idara za afya ili waendelee kuunganisha nguvu katika kusaidia jamii kampeni za mapambano dhidi ya virusi vya Covid-19. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwakuwepo na wataalamu wa kutosha katika maeneo yote, ambao wataendelea kutoa elimu ya kujikinga na kudhibiti ugonjwa wa corona usiingie mkoani Tabora. Mwanri alitoa kauli hiyo jana wilayani Uyui na Nzega wakati wa ziara yake ya kukagua vituo na zahanati zilizoandaliwa kwa washukiwa wa ugonjwa wa corona. Alisema kipaumbele hivi sasa ni kuhakikisha tahadhari zote zinachukuliwa ili wakazi wa Mkoa wa Tabora waendelee kuwa salama kwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya na viongozi wa kitaifa. Aidha Mwanri alizitaka halmashauri zote za Mkoa wa Tabora kutumia redio zilizopo na magari ya matangazo kupeleka elimu maeneo mbalimbali ya wananchi kuhusu kujikinga na virusi vya Covid-19. “Tumieni magari yenye vipaza sauti kupita katika mitaa mbalimbali kutoa elimu ya kujikinga wakati wote…na pia wataalamu nendeni katika redio zote zilizopo mkoani Tabora kupeleka ujumbe ambao utawasaidia wananchi kuepuka kupata maambukizi ya corona,” alisema Mwanri. Katika hatua nyingine, Mwanri ameziagiza halmashauri zote kuhakikisha magari yote yanayosafirisha abiria ndani na nje ya Mkoa wa Tabora yanapuliziwa dawa kabla ya safari ili kuwakinga abiria na uwezekano wa kupata corona. | 3 |
NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM USAJILI wa klabu ya Simba sasa umeziingilia timu za Azam FC na JKT Ruvu, baada ya juzi kunasa mabeki wawili wakitokea klabu hizo ili kuongeza uimara wa ukuta wa timu yao. Mabeki hao ni Samih Hajji Nuhu aliyekuwa mchezaji wa zamani wa Azam msimu wa 2013/2014 anayecheza beki ya kushoto ambaye wamempa mkataba wa mwaka mmoja na Mohammed Fakhi wa JKT Ruvu akiwa ni beki kati aliyeanguka saini ya miaka miwili. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya timu hiyo, Zacharia Hanspoppe alisema, uwezo wa wachezaji hao ndio umewafanya wawaongeze katika kikosi chao hicho. Alisema, usajili walioufanya hadi sasa ni kwa mapendekezo ya benchi la ufundi la timu hiyo kulingana na jinsi wao walivyoona uwezo wao kwani katika kipindi chote cha ligi licha ya kuhakikisha wanapata ushindi, pia walikuwa wakiangalia nani anawafaa kwenye usajili wa msimu ujao. “Kwa upande wa Nuhu ambaye alikuwa ni majeruhi tumejiridhisha na vipimo vyake na vimeonyesha ni mzima kabisa, hivyo tunategemea mambo mazuri kutoka kwao,” alisema. Usajili wa wawili hao umefanya idadi ya wachezaji wapya wa timu hiyo kufikia watatu, baada ya wiki iliyopita kumsajili kiungo wa Mbeya City, Peter Mwalyanzi. Makakati wa klabu hiyo ni kuacha wachezaji 10, saba wa ndani na watatu wa kigeni ambao tayari wameshajulikana huku bado kuna sintofahamu kuwa kati ya hao wa kigeni nani anaachwa na yupi anatolewa kwa mkopo. | 4 |
Na Tobias Nsungwe MWENYEKITI wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji, ni miongoni mwa wageni mashuhuri walioalikwa kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Rais Mteule wa Ghana, Nana Addo Dankwa Akufo-Addo na Makamu wake, Dk. Alhaji Mahamudu Bawumia. Sherehe za kuapishwa rais huyo zinatarajiwa kufanyika leo jijini Accra. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema makao makuu, Mbowe na ujumbe wake waliondoka nchini jana usiku. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, viongozi hao pia wanatarajiwa kushuhudia kuapishwa kwa Spika wa Bunge la Ghana. Pia wataona wabunge 275 waliopatikana baada ya Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana wakila kiapo. Taarifa ya Chadema pia ilisema Mwenyekiti Mbowe na Katibu Mkuu, Dk. Mashinji, watapata fursa ya kufanya mazungumzo na Rais Akufo-Addo yanayotarajiwa kufanyika kesho. Mbowe pia atapata nafasi ya kula chakula cha mchana na rais huyo mpya aliyetoka chama cha upinzani. “Kabla ya hapo, mapema asubuhi ya siku hiyo, viongozi wakuu wa Chadema watakuwa sehemu ya msafara utakaomsindikiza Rais Nana Akufo-Addo, kwenda kwenye ibada ya asubuhi, itakayofanyika eneo la Kyebi, kisha jioni msafara utarejea jijini Accra kuendelea na ratiba nyingine,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo. Taarifa pia ilisema ziara ya Mbowe nchini Ghana ni mwendelezo wa urafiki na uhusiano wa karibu kwa muda mrefu sasa kati ya Chama cha Rais Nana Akufo-Addo cha New Patriotic Party (NPP) pamoja na Chadema, tangu vilipokutanishwa kwenye Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia Duniani (IDU) na ule wa Afrika (DUA). Viongozi wengine mashuhuri kutoka Afrika walioalikwa katika sherehe hizo ni pamoja na Kiongozi wa Chama cha Forum for Democratic Change (FDC), Kizza Besigye, kutoka Uganda. | 3 |
TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazotarajiwa kunufaika na dola za Marekani milioni 120 zilizotengwa na Serikali ya Marekani kwa ajili ya utafi ti wa kupambana na ugonjwa wa selimundu (sickle cell). Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Brett Giroir alisema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi jijini New York, nchini Marekani. Brett aliutaja mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Kabudi kama mwanzo mpya wa ushirikiano baina ya Tanzania na Marekani na kuongeza kuwa nchi yake ina nyenzo zote ikiwemo teknolojia ya kupambana na maradhi ya selimundu ili kuboresha Maisha ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo. Waziri Kabudi alisema utafiti na hatimaye tiba ya maradhi hayo ya selimundu kwa kiasi kikubwa itainufaisha Tanzania kutokana na kushika nafasi ya tatu katika Bara la Afrika na ya nne duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wa selimundu. Aliongeza kuwa Tanzania na Marekani zitashirikiana kufundisha na kujengeana uwezo wa namna ya kupambana na maradhi ya selimundu lakini pia kutafuta fedha zitakazowezesha upatikanaji wa dawa ya selimundu kutokana na ukweli kuwa dawa za ugonjwa huo kwa Tanzania ni miongoni mwa dawa muhimu ili iweze kuwafikia wananchi wengi na kwa bei nafuu. Alizitaja nchi zilizo na idadi ya watoto wengi wanaozaliwa na ugonjwa wa selimundu ambapo kwa Afrika, Tanzania ni ya tatu baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Nigeria na ya nne duniani baada ya India. | 3 |
UJUMBE wa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ukiongozwa na Katibu Mkuu Taifa, Dk. Bashiru Ally umeondoka kwenda China kwa ziara ya kimkakati.Kwa mujibu wa taarifa ya Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na Idara ya Itikadi na Uenezi ya CCM, ziara hiyo imelenga kuongeza uhusiano kati ya CCM na Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China (CPC).Akizungumza kabla ya kuanza safari, Bashiru amesema safari hiyo ni ya kimkakati na inalenga kuimarisha mahusiano kati ya CCM na CPC.Aidha alisisitiza safari hiyo pamoja na mambo mengine ujumbe wa viongozi hao utakwenda kubadilisha uelewa, uzoefu na kujifunza mikakati ya kujitegemea kirasilimali ili kuendesha chama, namna bora na bunifu ya kuendesha Miji na Majiji nchini na namna bora ya kujenga uhusiano kati ya Chama na Serikali katika kutoa maendeleo kwa watu.Ujumbe wa Chama Cha Mapinduzi umejumuisha kwa uwakilishi viongozi wa Chama Taifa, ikiwamo wajumbe wa Baraza la Wadhamini, Jumuiya za Chama, Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Wajumbe wa Bodi za Kampuni za Chama na Maofisa wa Chama kutoka Ofisi Ndogo ya Makao Makuu.Chama Cha Mapinduzi katika ujumbe huu kimejumuisha maofisa wawili wa serikali ili nao wakajifunze kama sehemu ya ujumbe huo.Ujumbe wa CCM utakuwa nchini China kwa siku 10 na utakuwa na fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali wakiangazia fursa za mashirikiano na uwekezaji kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Taifa.Wakati huo huo, Bashiru amewashukuru wananchi wa Liwale kwa kufanya uchaguzi mzuri uliokamilika kwa amani na usalama na kuchagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia mgombea wake Zuberi Kuchauka. | 3 |
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya, alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele. “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema | 5 |
MANCHESTER, ENGLAND KIUNGO mshambuliaji wa timu ya Manchester City, Kevin de Bruyne, huenda akaukosa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Celtic, baada ya kupata jeraha katika mchezo dhidi ya Swansea ambapo timu yake ilipata ushindi wa mabao 3-1. Mbelgiji huyo mwenye thamani ya pauni milioni 56, jana alitarajia kufanyiwa uchunguzi wa jeraha lake baada ya kulalamika maumivu makali ya mguu katika mchezo huo. Hata hivyo, kocha wa timu hiyo, Pep Guardiola, hajawa na wasiwasi kumkosa nyota huyo wakati wakisafiri kuelekea jijini Glasgow, Scotland. Kocha huyo alisema kutokana na namna ambavyo nyota wake alivyokuwa akilalamika, inaonekana wazi alipata jeraha ya nyama za paja. “Sijajua jeraha hilo litakuwa kubwa kwa kiasi gani kwa kuwa mimi si daktari, tukifika Manchester atapatiwa uchunguzi ili kufahamu kitu kinachomsumbua. “Nasikitika sana kwani Kevin ni mchezaji muhimu katika timu yetu, hiyo ndio sababu ya kuwa na kikosi kipana,” alisema Guardiola. Manchester City iliwafunga kwa mara ya pili ndani ya wiki moja timu ya Swansea baada ya kuwafunga mara ya kwanza katika mchezo wa Kombe la Ligi ya England (EFL). Mshambuliaji wa timu hiyo, Sergio Aguero, alifunga mabao mawili katika mchezo huo wa EFL. Aguero kwa sasa amefunga mabao 11 katika michezo sita msimu, huu hata hivyo Guardiola anataka nyota huyo kujituma zaidi uwanjani. Kocha huyo alimpongeza nyota huyo baada ya ushindi huo na kumweleza kuwa anaweza kufanya vizuri zaidi ya ushindi wa mabao hayo. | 4 |
Aveline Kitomary Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza ongezeko la wagonjwa wenye maambukizi ya corona 196 nchini, Tanzania Bara ikiwa na wagonjwa 174 na Zanzibar wagonjwa 22 ambao walitolewa taarifa na Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid na kufanya idadi ya wagonjwa wa corona nchini kufikia 480.Majaliwa amesema hayo leo Jumatano Aprili 29, jijini Dodoma wakati akigawa magari 50 ya kubebea wagonjwa kwa wabunge wa majimbo mbalimbali.Amesema jumla ya wagonjwa waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi kufikia 197, huku Zanzibar waliopona wakiwa 36 na Tanzania bara 83.“Kumekuwa na ongezeko la vifo vya watu sita na hivyo kufanya idadi ya vifo vilivyotoka na corona nchini kufikia 16. “Kati yao wenye maambukizi 297, waliobaki 283 wanaendelea vizuri na tiba na kusubiri ufuatiliaji wa afya zao na wengine 14 wako chini ya uangalizi maalumu wa madaktari ambao wanahitaji oksjeni ya kuwasaidia kupumua pamoja na wale wenye magonjwa mengine ambayo yamejitokeza kwenye wodi.“Serikali imeendelea kuwaondoa washukiwa waliokuwa karantini ambao walishatimiza siku 14 baada ya uchunguzi wa kiafya kuonekana hawana maambukizi na kuruhusiwa kurudi nyumbani,” amesema.Majaliwa amesema hadi kufikia jana Aprili 28, watu 644 wameruhusiwa kutoka karantini katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Arusha, Zanzibar, Kilimanjaro, Mwanza, kagera, Songwe, Kigoma na Dodoma. Hata hivyo, Waziri Mkuu amekemea tabia ya upotoshaji na utoaji wa takwimu ambazo si rasmi na kuzua taharuki kwa jamii kwamba kila kifo kimetokana na Corona kuwa si sahihi na kusisitiza kuwa kuna magonjwa mengine ambayo yanaua pia. | 0 |
RAIS John Magufuli ameungana na Watanzania kumkumbuka hayati Abeid Amani Karume kwa kutaka vijana kusoma historia waelewe mchango wa waasisi wa taifa na mapinduzi ya kweli waliyofanya.Katika hatua nyingine; mamia ya wananchi wakiongozwa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein wamehudhuria katika ibada ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Shehe Abeid Amani Karume, Kisiwandui mjini Unguja.Wosia wa Rais MagufuliAkihutubia mkutano wa hadhara katika eneo la Makita mjini Mbinga baada ya kuweka jiwe la msingi ya ujenzi wa barabara ya Mbinga-Mbamba Bay, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Ruvuma jana, Rais Magufuli alisema taifa lipo kutokana na michango mikubwa ya Karume na Mwalimu Julius Nyerere.“Tunapokumbuka kifo cha Karume, nitoe mwito kwa vijana waliozaliwa baada ya kifo chake, wakaisome historia ya taifa. Wakayasome mapinduzi ya taifa la Zanzibar na mapinduzi ya kweli ya nchi yaliyoweza kuzaa taifa la Tanzania,” alisema.Alisema: “Leo ni siku ya Karume ambayo inasherehekewa katika nchi nzima. Viongozi wenzangu wako Zanzibar; Mimi nilifikiri pamoja na viongozi wengine niliokuja nao tuisherehekee tukiwa hapa Mbinga.“Tunaisherehekea kwa kutambua kazi kubwa iliyofanywa na mwanamapinduzi huyu. Alikuwa mchapakazi, alipenda watu, alijituma, alipenda umoja, mshikamano na aliwakilisha vyema watanzania ,” alisema.Alisisitiza kuwa kikubwa zaidi, Karume alikuwa mchapakazi na ndiyo maana ameona katika kusherehekea aanze kushughulika na miradi ikiwa barabara hiyo ya Mbamba-Mbamba Bay itakayogharimu Sh bilioni 134.72.Alisema daima taifa litaendelea kumkumbuka mwanamapinduzi huyo pamoja na Mwalimu Nyerere kwa kuiweka nchi kwenye ramani ya dunia. Alisema waasisi hao waliipenda Tanzania na kwamba uthibitisho wake ni nyumba alizojenga kabla ya mwaka 1972 .“Tangu aondoke hakuna majengo mengine yaliyojengwa. Hawa walikuwa ni wana mapinduzi,” alisema na kumtaja pia Nyerere kwa kujenga viwanda kila mahali akisema dhamira na mawazo yao yalikuwa mazuri.Aliomba watanzania kuendelea kuenzi kazi nzuri zilizofanywa kwa kukumbuka, kujifunza na kutekeleza mazuri yaliyofanywa na hasa ulinda na kutunza muungano.Kisomo cha kumuombea Zanzibar Ibada ya kisomo cha hitma iliongozwa na Mufti wa Zanzibar, Shehe Saleh Kabi ambaye alimtaja hayati Karume kuwa kiongozi wa kupigiwa mfano katika kuwatumikia wananchi wa Zanzibar.Shehe Kabi alisema Karume alishika madaraka katika kipindi kifupi cha miaka tisa, lakini mambo aliyoyafanya kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar ni makubwa sana huku mifano yake ikionekana wazi wazi.“Tunamuombea dua kiongozi na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Shehe Karume ambaye alifanya mambo makubwa kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar ambapo Mungu atamlipa malipo mema,” alisema.Mara baada ya kumaliza kisomo cha Khitma viongozi mbalimbali waliweka mashada ya maua katika kaburi lake lililopo pembezoni mwa jengo la lililokuwa Makao Makuu ya ASP sehemu ambayo kiongozi huyo aliuawa kikatili. Rais wa Zanzibar, Dk Shein aliongoza uwekaji wa mashada ya maua katika kaburi hilo akifuatiwa na Makamu wa Rais wa Muungano, Samia Suluhu Hassan.Aidha Meja Jenerali Sharif Othman aliweka shada la maua kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWT).Wengine waliopata fursa hiyo ni mwakilishi wa wazee Hamadi Ussi Haji kutoka kisiwa cha Tumbatu Mkoa wa Kaskazini Unguja na Mwakilishi wa Mabalozi waliopo Zanzibar waliwakilishwa na Balozi Mdogo wa Msumbiji, Jorge Augusto Menezez. Waziri wa Vijana, Balozi Ali Karume aliwakilisha familia ya wazee katika kuweka shada la maua katika kaburi la baba yake mzazi.Katika kumbukumbu hiyo pia viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano walihudhuria akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, January Makamba.Wengine ni Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally.Wakihojiwa kwa nyakati tofauti, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud aliwataka Wazanzibari kuimarisha umoja na mshikamano ambao ni hazina kubwa waliyoachiwa na hayati Karume.“Karume aliuawa na kuzikwa lakini baadhi ya mambo makubwa aliyotuachia ambayo ni hazina kubwa ni amani na mshikamano,” alisema.Mjane Fatma Karume alisema anachokikumbuka kikubwa kutoka kwa mumewe ni ukarimu kwa watu mbalimbali na kufanya kazi kwa kuwatumikia watu wengine.“Karume amekufa na kuziacha nyumba za maendeleo ambazo alitumia muda mwingi kuzijenga huku zikiwanufaisha watu wengine..... hicho ndicho kigezo cha kiongozi anayetakiwa na wananchi,” alisema.Karume aliuawa Aprili 7, 1972 katika Makao Makuu ya ASP Kisiwandui akiwa na viongozi wengine wakicheza mchezo wa Dhumna ambapo walivamiwa na kushambuliwa kwa kupigwa risasi.Wadau Dar wammwagia sifaKatika hatua nyingine Watanzania wameaswa kumuenzi Hayati Abeid Amani Karume kwa kusimamia yale aliyoyasimamia ikiwemo uhuru, uzalendo, kujituma, kufanya kazi, ikiwa ni pamoja na kuridhika na kile mtu anachokipata.Mbunge wa Vitu Maalumu Zanzibar, Asha Abdalah Juma alisema jana katika kipindi Maalumu kilichorushwa na TBC cha Kumbukizi ya miaka 47 ya kifo cha Karume.Alisema Karume alikuwa ni kiongozi wa hali ya juu mwenye uthubutu na kumfananisha na Rais Magufuli ambaye amekuwa akitetea wananchi wanyonge.“Ukitaka kuleta maendeleo inabidi uwe mkali na mfuatiliaji. Rais Magufuli anavyokwenda atatupeleka mbali.“Miaka 10 ijayo ya Magufuli tutakuwa mbali, tutakuwa juu. Sasa hivi vitu vinakwenda kwa haraka kutokana na miradi mikubwa mbalimbali inayoendelea,” alisema.Akimzungumzia Karume ambaye alikuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, alisema alibadili hali ya wananchi wa Zanzibar kwa kufanya uwepo wake kuwa rasmi Machi 8, 1964. Alisema Rais huyo alifanikiwa kutangaza rasmi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Uzanzibari na ardhi kuwa ni mali ya umma kwa kuwa hayo yote yalikuwa hayapo wakati huo.“Kulikuwa na ubaguzi sana katika elimu akatangaza elimu bure. Wote walipata nafasi ya kusoma kwa maana kikwazo kilichokuwepo kiliondoka,” alisema.Kwa upande wake Spika mstaafu Pius Msekwa alimwelezea Karume kuwa alikuwa kiongozi wakati naye ni kiongozi.Alisema Karume alikuwa makini, mzalendo, mpenda nchi yake naye na Mwalimu Nyerere waliweza kushirikiana vizuri katika kuutengeneza na kuunda Muungano.Alisema Karume na Nyerere ndio waliweka msingi ambao unadumu mpaka hivi leo. Naye Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema anamwelezea Karume kama muasisi wa Muungano na baba wa mageuzi hivyo fikra zake zinaendelea kwani amekufa kimwili lakini kiroho yupo na Watanzania.Alisema msingi wa Muungano ulitokana na Karume alipokutana na Nyerere, kwani si rahisi kukubali kuwa Makamu wa Rais na kumwacha Nyerere awe Mwenyekiti.“Aliweka maslahi mbele kwa kuutaka Muungano. Unaposikia watu wanataka kuuvunja Muungano tuwazuie tusikubali kwani ni walafi wa madaraka. Hicho ndicho kinachomfanya Karume awe juu kwenye mioyo ya watu ni mfano wa kuigwa,” alisema.Alisema kama si Karume kisiwa cha Zanzibar na Pemba kingeshatekwa kwani maadui wa Muungano bado wanatafuta nafasi kwa sababu bado kuna chokochoko za Muungano.Alisema masalia ya wanaopinga muungano yanaingia kwa sura mbalimbali ikiwemo kupitia vyama vya siasa hivyo ni vema kumuunga mkono Karume kwa kudumisha Muungano huo.Imeandikwa na Khatib Suleiman, Zanzibar, Stela Nyemenohi na Lucy Ngowi, Dar. | 3 |
Hayo yalisemwa na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Mazrui wakati alipozungumza na wajasiriamali walioshiriki katika Maonesho ya Siku ya Wafanyakazi duniani Mei Mosi yaliyofanyika katika viwanja vya Amaan.Alisema miongoni mwa njia zitakazowawezesha wajasiriamali kuonesha bidhaa zao na kuziuza ni kufanya maonesho ya kibiashara yatakayohudhuriwa na wananchi mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara.“Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko imefungua milango kwa wajasiriamali na taasisi mbalimbali kuandaa Maonesho ya kibiashara yatakayotangaza biashara zao na kupata soko,” alisema.Kwa mfano alisema Maonesho ya Mei Mosi yalionesha kwamba taasisi na wajasiriamali mbalimbali na taasisi wanao uwezo wa kutangaza bidhaa zao wanazotengeneza au kuzalisha.“Nimefurahishwa na bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali mbalimbali ambazo zimetengenezwa na wafanyabiashara,” alisema.Baadhi ya bidhaa zilizooneshwa na wajasiriamali na kuonesha ubunifu mkubwa ni utengenezaji wa zao la mwani kwa matumizi mbalimbali ikiwemo keki na mkate.Mmoja ya wajasiriamali wanaozalisha na kutengeneza zao la mwani kwa matumizi mbalimbali ikiwemo keki, Bimkubwa Haji alisema zao la mwani limeongezeka thamani yake kufuatia kuongezeka kwa matumizi mbalimbali. | 5 |
TEKNOLOJIA ya Habari na Mawasiliano (Tehema) imeelezwa kuwa ni muhimu kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ikiwemo afya, elimu na usawa wa kijinsia.Kutokana na umuhimu huo, serikali, wafanyabiashara na asasi za kiraia zinapaswa kufanya kazi kwa pamoja kutokana na maendeleo ya Tehama. Akizungumza wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Uchukuzi, Habari na Hali ya Hewa wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Makamu wa Rais wa Huawei Ukanda wa Kusini mwa Afrika, David Chen, alisema kuna uhusiano mkubwa kati ya Tehama na kiwango cha maendeleo kwenye SDGs.Chen alisema uhusiano huo hujidhihirisha hasa katika malengo ya maendeleo endelevu namba 3, 4, 5 na 9 kuhusu elimu bora, afya bora na ustawi, usawa wa kijinsia na viwanda, uvumbuzi na miundombinu.“Maendeleo ya pamoja ya kidijiti yanahitaji ushirikiano wa kipembe tatu kati ya sekta ya umma, sekta binafsi na asasi za kiraia.Serikali inahitaji sera madhubuti na kutumia sera hizo kupunguza gharama za matumizi ya Tehama ambayo itasababisha kuongezeka kwa huduma za kidijiti kwa gharama nafuu,”alisema Chen. Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, asilimia 53 ya watu duniani bado hawatumii mtandao wa intaneti, lakini pia 4/5 ya watu ambao hawajaunganishwa na mtandao wa intaneti wanapatikana katika ukanda wa Asia-Pacific na Afrika. Imeelezwa kuwa Afrika inaupungufu zaidi ikizingatiwa kuwa sehemu kubwa ya watu wake bado hawajaunganishwa kimtandao. Kwa wastani, asilimia 76 ya watu Afrika hawajaunganishwa na huduma ya intaneti na wengi wao wako maeneo ya vijijini. Kutokana na hali hiyo, Chen alisema Septemba 18 mwaka huu Huawei ilitangaza mpango wake jumuishi wa kidijiti ujulikanao kama TECH4ALL huko Shanghai kwa lengo la kuwasaidia watu wengine milioni 500 kunufaika na teknolojia ya kidijiti katika miaka mitano ijayo.Kampuni hiyo ya Huawei imetoa wito kwa watu binafsi na mashirika kuungana nao katika kushughulikia mambo ya kidunia yanayohusiana na afya, elimu, maendeleo na mazingira.Alisema katika kufikia mpango jumuishi wa kidijiti wa TECH4ALL, Huawei iliweka bayana hivi karibuni mradi wake ujulikanao kama DigiTruck Afrika kwa kushirikiana na shirika lisilotengeneza faida la Ubelgiji ili kuwapatia mafunzo ya kuwaongezea ujuzi jamii za vijijini nchini Kenya. | 5 |
NAIROBI, KENYA
RAIS wa Kenya, Uhuru Kenyatta, ameomba radhi kwa kutojiandaa na mwitikio mkubwa wa wapiga kura uliolazimisha kufutwa kwa uchaguzi wa mchujo wa chama chake nchi nzima.
Kenyatta alisema chama cha Jubilee kitafanya uchaguzi mpya wa mchujo leo na kesho.
“Viongozi hawakutarajia mwitikio mkubwa wa watu kujitokeza kupiga kura na kusababisha upungufu wa karatasi za kura,” alisema.
Hilo lilisababisha vurugu kote nchini wakati wagombea walipowatuhumu wenzao kwa uchakachuaji.
Kenyatta alitarajia mwitikio wa asilimia 25 lakini uliotokea ulikuwa wa zaidi ya asilimia 70.
“Kura za mchujo kwa kawaida hazivuti mwitikio mkubwa wa wapiga kura kama tulioshuhudia Ijumaa iliyopita na hapo inaonesha hatukuwa tumejiandaa vyema," alisema.
Kati ya kaunti 21, ambazo kura za mchujo zilikuwa zifanyike, ni chache zilizoweza kuendesha.
Mchakato huo unafanyika kupata wagombea wa chama watakaochuana na wenzao pinzani wakati wa uchaguzi mkuu wa Agosti, ambapo pia rais mpya atachaguliwa.
Mwongo uliopita, watu zaidi ya 1,300 walikufa katika machafuko yaliyotokana na uchaguzi wenye utata, lakini wa karibuni uliofanyika mwaka 2013 ulikuwa wa amani. | 2 |
MOHAMED KASSARA-DAR ES SALAAM KIKOSI
cha Wekundu wa Msimbazi, Simba leo kitashuka dimbani kumenyana na Mbeya City, katika
mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Simba
itashuka dimbani ikiwa na jeraha ililolipata baada ya kupoteza mchezo wake
uliopita dhidi ya Mwadui ya Shinyanga, ilipokubali kichapo cha bao 1-0, mchezo
uliochezwa Uwanja wa Kambarage. Mabingwa hao watetezi wa taji hilo, bado wanaendelea kushikilia usukani, wakiwa na pointi 18 walizovuna baada kucheza
michezo saba, wakishinda sita na
kupoteza mmoja. Mbeya City wanayokutanayo, inashika nafasi ya 16 miongoni mwa timu 20
zinazochuana, ikiwa na pointi nane, ilivovuna baada ya kucheza michezo nane,
ikishinda mara moja, sare tano na kupoteza mara mbili. Wagonga Nyundo hao wa Jiji la Mbeya,
wana kiu ya kuvuna pointi tatu, kwani mchezo wao uliopita walilazimisha suluhu
na Alliance, Uwanja wa Nyamagana, Mwanza. Lakini rekodi zinaipa nafasi kubwa Simba
ya kuibuka mbabe. Katika michezo miwili ambayo timu
hizo zilikutana msimu uliopita, Simba ilikomba zote. Ikianza kushinda mabao 2-0 nyumbani
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kabla ya kupata ushindi wa mabao 2-1, Uwanja
Sokoine, Mbeya. Mbeya City inayofundishwa na kocha,
Juma Mwambusi, imekuwa ikisuasua tangu
msimu huu umeanza. Lakini Mwambusi ana rekodi chanya
dhidi ya Simba, kwani msimu wake wa kwanza akiwa na Mbeya City hakuwahi
kupoteza. Mbeya City ilianza kuilazimisha
Simba sare ya bao 1-1 Uwanja wa Taifa, kabla ya kupata matokeo kama hayo Uwanja
wa Sokoine. Simba itakuwa imesheheni, baada ya nyota wake watatu waliokuwa majeruhi
kurejea kundini, hawa ni nahodha John Bocco na mabeki Shomari Kapombe na
Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, waliokosekana mechi mbili zilizopita. Kocha
Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema wana kila sababu ya kuondoka na pointi
tatu kwa kuwa watacheza kwenye uwanja ambao wameuzoea. “Tunacheza
nyumbani tena kwenye uwanja ambao tumeuzoea, “Ikiwezekana
tufunge mabao mengi kwa sababu tutakuwa katika eneo letu la kujidai, Uwanja wa
Uhuru ambao tumeuozoea tofauti na viwanja vya mikoani,” alisema. Kwa
upande wake, Mwambusi alisema amejipanga vilivyo kukabiliana na Simba na lengo
lao kubwa ni kuhakikisha hawatoki mikono mitupu. Mbali
na mchezo huo, kivumbi kingine cha ligi hiyo kitatimka Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara ambapo, Ndanda FC itakuwa
nyumbani kupambana na Ruvu Shooting,Polisi Tanzania itaikaribisha Alliance FC,
Uwanja wa Chuo cha Ushirika, Moshi. | 4 |
NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeamuru jalada la kesi ya vigogo wa Chadema, akiwamo Mwenyekiti Freeman Mbowe, waliokata rufaa kupinga kutiwa hatiani na adhabu lirejeshwe Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kukusanya mwenendo mzima wa kesi hiyo. Uamuzi wa mahakama hiyo ulitolewa jana mbele ya Jaji Ilvin Mgeta baada mlalamikiwa Jamhuri kudai kwamba wamepokea mwenendo wa kesi, lakini kuna nyaraka zingine hazipo. Akiwawakilisha warufani, Wakili Peter Kibatala alidai kuwa walalamikaji watano; Mbowe, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu, Visiwani Zanzibar, Salum Mwalimu, Katibu Mkuu John Mnyika na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche walikuwepo mahakamani. Kibatala alidai kuwa walalamikaji, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko, Halima Mdee (Kawe) na Esther Bulaya (Bunda) wameshindwa kufika mahakamani kwa sababu ya matatizo ya afya zao. Alidai kuwa walalamikaji wameridhia rufani hiyo kuendelea kusikikizwa bila uwepo wao. Upande wa wajibu rufani ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraji Nchimbi akisaidiana na Wakili wa Serikali Salimu Msemo, ulidai kuwa kuendelea kusikiliza rufani bila uwepo wa walalamikaji watatu hawana pingamizi, wanaiachia mahakama. Hoja ya walalamikiwa inajikita kwamba nyaraka walizopatiwa na Mahakama Kuu haziko sawa, zina kasoro ili waweze kuitetea rufani ya walalamikiwa dhidi yao. Nchimbi alidai kuwa hatua za usikilizwaji zilipitia mahakimu wawili tofauti na zilitakiwa kuwa na kurasa kati ya 566 au zaidi. Akijibu hoja za walalamikiwa, Kibatala alidai kuwa mawakili wote walishiriki kesi hiyo tangu inaanza mbele ya Jaji Wilbard Mashauri (wakati huo akiwa hakimu). Alidai kuwa wao ni maofisa wa mahakama na Aprili 28, mwaka huu Jaji Mfawidhi, Lameck Mlacha rufani hiyo ilipotajwa mbele yake aliwauliza kama kuna lolote lakini pande zote mbili zilieleza ziko tayari kuanza kusikiliza jana. “Mei 11, mwaka huu nilipata barua kutoka kwa Jaji Mfawidhi akisistiza kwamba tufike mahakamani kwa ajili ya kusikiliza rufani hiyo. “Tunapinga maombi ya walalamikiwa ya kutaka ahirisho, mahakama iwe na ukali kusimamia amri zake, kama itaahirishwa iwe kwa muda mfupi ili tuendelee na kusikiliza rufani hii,” alidai Kibatala. Jaji Mgeta alisema mahakama yake imepokea majibu ya barua ya Mei 11, mwaka huu kutoka kwa walalamikiwa, wakielezea kasoro zilizopo kwenye mwenendo wa kesi hiyo kutoka Mahakama ya Kisutu. “Mfano hakuna mwenendo wa Februari 24, mwaka huu na kuendelea,” alisema Jaji Mgeta. Akitoa uamuzi, alisema kama kuna mwenendo wa mahakama nyingine tofauti na Kisutu utengwe pembeni. Alisema mahakama yake inaamuru jalada hilo kurejeshwa Mahakama ya Kisutu, ikakusanye mwenendo jana na leo, kuanzia kesi ilipoanza hadi mwisho wa hukumu yake. “Naagiza jalada hili lirejeshwe Mahakama ya Kisutu leo na kesho (jana na leo) wakakusanye mwenendo tangu kesi ilipoanza mpaka ilipotolewa hukumu. “Ijumaa Mei 15, mwaka huu jalada lirejeshwe hapa ili pande zote mbili mpate nakala za mwenendo huo, Jumatatu Mei 18, mwaka huu tukutane hapa saa tatu asubuhi kuanza kusikiliza,” alisema Jaji Mgeta. Mbowe na wenzake wamekata rufani Mahakama Kuu kupinga hukumu ya kulipa faini ya jumla ya Sh milioni 320 au kwenda jela miezi mitano kwa kila kosa. Rufani hiyo iliyosajiliwa kwa namba 76 mwaka huu imewasilishwa na Kibatala ikiwa na sababu 14. Kwa mujibu wa hati ya rufani, walalamikaji wanadai kuwa Mahakama ya Kisutu ilikosea kuwatia hatiani Mbowe na wenzake kwa sababu haikuchambua ushahidi wa Jamhuri wakati wa kuandika hukumu hiyo. Hoja nyingine, Mahakama ya Kisutu katika hukumu yake haikuonyesha sababu zilizosababisha washtakiwa kutiwa hatiani. “Upande wa Jamhuri ni jukumu lao kuthibitisha makosa bila kuacha shaka na kwamba si kazi ya mshtakiwa kujitetea,” ilieleza sehemu ya hoja za walalamikaji. Hoja nyingine, Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba hakutilia manani utetezi wa washtakiwa Matiko na Mnyika kwamba katika ushahidi wa Jamhuri hakuna ulipoeleza kama walikuwepo kwenye tukio. Kwamba pia mahakama ilikosea kuwatia hatiani washtakiwa katika shtaka lililokuwa na mashtaka manne ndani yake ikiwamo kufanya maandamano, kusababisha kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwiline na askari polisi wawili kujeruhiwa. Hoja nyingine ni kwamba mahakama ilipokea CD iliyoonyesha maandamano ya washtakiwa kinyume cha sheria na kwamba utaratibu wa kisheria haukufuatwa na kielelezo hicho kilipokewa kiholela. Katika kesi ya msingi, Mbowe na viongozi wenzake walishtakiwa kwa mashtaka 12 ya uchochezi na moja la kula njama. Mashtaka 12 yaliyowakabili, katika shtaka la kula njama, walidaiwa kati ya Februari Mosi na 16, mwaka 2017, wakiwa Kinondoni Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama na wengine ambao hawapo mahakamani kwa kutenda kosa la jinai na kuendelea na mkusanyiko isivyo halali na kusababisha chuki na uchochezi wa uasi. Bulaya alikabiliwa na shtaka la kushawishi kutenda kosa la jinai ambapo alidaiwa Februari 16, mwaka huo, katika viwanja vya Buibui Kinondoni, Dar es Salaam alishawishi wakazi wa Kinondoni kutenda kosa la jinai kwa kufanya maandamano yenye vurugu. Washtakiwa wote Februari 16, mwaka huo, wakiwa katika barabara ya Kawawa, Kinondoni Mkwajuni, Dar es Salaam, kwa pamoja wakiwa wamekusanyika kutekeleza lengo la pamoja kinyume cha sheria, waliendelea na mkusanyiko katika namna iliyowafanya watu waliokuwa kwenye eneo hilo waogope watakwenda kwenye uvunjifu wa amani. | 3 |
Kulwa Mzee, Dar es Salaam Mhasibu Mkuu wa Klabu ya Simba, Amos Juma amedai aliyekuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange (Kaburu) walihamishia Dola za Marekani 300,000 zilizotokana na kumuuza mchezaji Emmanuel Okwi katika Klabu ya Tunisia kwenye akaunti ya Aveva. Juma amedai hayo leo asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba. Akiongozwa na Wakili wa Serikali kutoka Takukuru, Leonard Swai, shahidi huyo amedai Machi 14,2016 kiliitishwa kikao cha Kamati ya Utendaji cha kawaida kikiwa na ajenda 10 ikiwemo ajenda moja ya fedha zilizoingia kwa mauzo ya mchezaji Okwi ambayo ni ajenda ya Saba. “Juni 16,2016 nikiwa ofisini kwangu, Kaburu alikuja kuomba nimpe kitabu cha hundi ya akaunti ambayo fedha za Okwi ziliingizwa, nilimpa lakini alipokirudisha karatasi mbili hazikuwepo. “Alinikabidhi kipande cha karatasi kikionesha kuna Dola za Marekani 300,000 zilihamishiwa katika akaunti ya Aveva, karatasi hiyo ilitoka Benki ya CRDB,” amedai mhasibu huyo. Katika kesi ya msingi, inadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Machi 10 na 16, 2016 Aveva na Kaburu walikula njama ya kutenda kosa la matumizi mabaya ya ofisi na kutakatisha fedha. Mwisho | 4 |
KAMPUNI ya Ndege Tanzania (ATCL) imezindua tovuti ya kampuni hiyo inayotoa fursa kwa wateja wake kupata huduma kwa urahisi na kutangaza safari zake katika nchi za Zimbabwe na Zambia.Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi alisema hayo jana jijini Dar es Salaan wakati wa uzinduzi tovuti hiyo ya mauzo ya masoko ya kampuni hiyo. Matindi alisema wameboresha mfumo wa kutoa huduma ili kuwarahisishia wateja ambao wanahitaji huduma za kampuni hiyo kongwe ya ndege ya umma. “Haya ni baadhi ya mambo ambayo tulijipangia katika mpango kazi wetu wa miaka mitano, kuboresha huduma, tunatarajia kuanza safari za Zimbabwe na Zambia mwezi huu na nyingine Machi,” alisema.Alisema kwa kupitia kompyuta au simu ya kiganjani, mtu anaweza kuingia katika tovuti hiyo na kuchagua safari, kukata tiketi ya safari anayoitaka na kufanya malipo. “Sasa tuko nyumbani kwako, ofisini kwako na popote ulipo,” alieleza. Alisema mbali na hatua hiyo, ATCL pia inatarajia kuanza kufanya safari zake kwenda Afrika Kusini, India na China ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao. Alisema ATCL imetangaza safari za Bara la Asia katika miji ya Bombay nchini India na China na sasa inaanza kwenda miji ya Lusaka nchini Zambia na Harare, Zimbabwe na Johannesburg, Afrika Kusini.Aidha, alisema ATCL ilikuwa inapambana kuingizwa katika Mfumo wa Malipo wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (IATA) ambao sasa wamekamilisha hivyo safari za masafa marefu zitaongezeka. “Sasa tiketi zetu zinauzwa duniani kote na kuuzwa na wakala popote ulipo, tulikuwa tumesimamishwa IATA, lakini kwa sasa tumesharudishwa kwenye uanachama,” alisema Matindi.Matindi aliwataka mawakala wa ndege za ATCL kuitumia fursa hiyo vizuri kuitangaza na ATCL iko tayari kuwawezesha. Alisema wanatarajia kuongeza muda wa kufanya kazi kuwa saa 14 kuelekea saa 24 na pia kuwawezesha wateja wake kulipia huduma mtandao wakati wowote kupitia mitandao ya simu na kupitia benki. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ATCL, Emmanuel Korosso aliwaomba mawakala wa ATCL mbali na kuuza tiketi, waitangaze kampuni kwani asilimia 90 ya tiketi zao ni wao wanaziuza. Korosso alisema kwa kuitangaza, ATCL itapata mafanikio na wao watanufaika. | 3 |
KAMPUNI ya ndege Tanzania (ATCL) imesema haijaajiri wazee kutoa huduma kwenye ndege na pia wote wanaofana kazi hiyo wana sifa za kitaaluma kwa kuwa utaratibu wa kuwapata, umezingatia matakwa ya kimataifa yanayohusiana na kazi hiyo na si urembo wao.Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi amesema jijini Dar es Salaam kuwa, kimsingi wahudumu wa ndege hizo, wameajiriwa kutokana na sifa sambamba na kuwa na viwango vinavyotambuliwa na Mamlaka ya Usalama Anga (TCAA).Amesema, ATCL ina wahudumu wa kike na wa kiume, na wote urefu wao haupungui futi 5.2 na kwamba urefu huo ni kwa mujibu wa sheria, kanuni na aina ya ndege zao na kwa kuzingatia sheria za kimataifa.Kwa mujibu wa Matindi kuhudumia ndani ya ndege ni taaluma yenye vigezo na masharti na kwamba, ATCL inazingatia hilo"Kwa hiyo tunapozungumzia uzuri ni ule uwezo wa kufanya ile kazi, kwangu ndiyo definition (maana) ya uzuri, uwezo wa kufanya ile kazi na ile haiba ambayo tumeieleza sie, urefu wa chini futi 5.2, uzito upo umeelezwa kabisa body mass index yaani uwiano wa urefu na uzito wa mtu, upo umeelekezwa na hii ni kwa sababu aweze kufanya kazi zake bila matatizo sio awe aende akafanye catwalk, siajiri catwalkers, hapana." amesema MatindiAlisema ATCL inatekeleza Mkataba wa Kimataifa wa Chicago, unaoelezea viwango mbalimbali wanavyohitajika kuwa navyo watoaji wa huduma za ndege, huku ikizingatia viwango vya urefu vya wahudumu hao na mafunzo waliyopata tayari, kukabiliana na hali yoyote inayoweza kujitokeza wakati wa safari.“Mhudumu anayepaswa kufanya kazi hizi, kwanza anapaswa kuwa mwenye uwezo wa kumiliki vifaa vyote vya usalama ndani ya ndege mbali na uzoefu wa kuogelea, kwa kuwa jukumu lake ni kuhakikisha anamsaidia msafiri kwa hali yoyote pale majanga yanapotokea,” alisema Matindi.Kauli ya Mkurugenzi huyo, imekuja siku chache tangu kutolewa hoja na mmoja wa wabunge bungeni, aliyesema kuwa wahudumu wa ndani ya ndege za kampuni ya ATCL, hawana mvuto kutokana na kutokuwa warembo, ikilinganishwa na mashirika mengine ya ndege na hivyo kuzua mjadala."Tuna experienced cabin crew na lazima uwe na experience hiyo, unajua kutengeneza hao mabinti wazielewe kazi, kuwe na nidhamu kwenye ndege na kila kitu kwa hiyo ni taaluma, ni taaluma yenye masharti na vigezo, kuna kigezo cha uzuri kinazungumzwa, mimi uzuri siwezi nikau-define, sijui nyie waandishi kama mnajua, nani mzuri kati yenu hapa ajitokeze aseme uzuri ni mimi, ukitaka kuajiri ukisema uzuri ni mimi"amesema Matindi.Hata hivyo, Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Atashasta Nditiye alitoa ufafanuzi kwa mbunge huyo, kwa kueleza kuwa suala la wahudumu wanaohitajika kufanya kazi katika ndege hizo, linasimamiwa zaidi na taaluma na siyo urembo wao.Akisisitiza majibu hayo, Mkurugenzi huyo wa ATCL alisema kama mahitaji ya wahudumu wa ndege hizo, yangekuwa yanahusu urembo wao, wangeweza kuwaajiri washiriki wa mashindano ya urembo, kufanya kazi katika ndege hizo.Lakini, siyo hivyo, ndiyo maana wamewaajiri wahudumu wenye vigezo vinavyotambuliwa kimataifa.Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo alisema tangu kuanzishwa kwa safari za ndege kwenda mkoani Katavi, kumekuwa na mwitikio mkubwa wa abiria na kuifanya ndege hiyo inayofanya safari mara moja kwa wiki kujaa kila wakati.Alisema kutokana na hatua hiyo, wanatarajia kuongeza safari za ndege hiyo ifikapo Desemba mwaka huu baada ya kuwasili kwa ndege zingine mbili kati ya mwezi huu na Desemba. | 5 |
Na WAANDISHI WETU-DAR
VYAMA vya siasa pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya haki za binadamu nchini, wamemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini kutafuta kiini cha mauaji ya askari polisi ambayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, walisema shambulio dhidi ya askari wanane lililotokea juzi ni hatari na kwamba linatishia usalama wa raia na mali zao.
Kuali ya THBUB
Kwa upande wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imesema imepokea kwa masikitiko na kulaani vikali tukio hilo.
Taarifa iliyotolewa jana na Mwenyekiti THBUB, Bahame Nyanduga, imeeleza kuwa mauaji hayo ya kikatili yametokea kwa askari polisi wasiokuwa na hatia waliokuwa kazini.
“Kumbukumbu zinaonyesha kuwa matukio ya mauaji ya askari polisi na wananchi wengine maeneo tofauti mkoani Pwani tangu mwaka 2015 yamekuwa yakiongezeka na kusababisha uvunjifu wa haki za binadamu, hususani haki ya uhai inayolindwa na Katiba ya nchi na madhara mengine kwa familia za wahanga, kwa jamii na Taifa kwa ujumla.
Alisema ikumbukwe kwamba, askari polisi wanapokuwa kazini wanatekeleza majukumu muhimu ya kulinda raia na mali zao, kwa hiyo usalama wao unategemewa na Watanzania wote.
Aliongeza yeyote yule anayewaua askari polisi si tu anataka kuwachonganisha askari polisi na raia, bali pia anawaweka raia hao katika hofu kubwa ya usalama na mali zao.
Alisema kutokana na hali hiyo, tume inashauri katika kuhakikisha kuwa haki ya kuishi ya askari polisi na wananchi wote inalindwa na Jeshi la Polisi na Serikali kwa ujumla, wafanye uchunguzi wa kina ili kubaini sababu za mauaji haya kujirudia mkoani Pwani.
Alisema polisi wanapaswa kuhakikisha wahusika wote wanapatikana na wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake.
Kauli ya THRDC
Wakati huo huo Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini (THRDC), umesema mauaji hayo yanatishia usalama wa wananchi na mali zao na endapo yataendelea usalama wao utakuwa shakani.
Akizungumza jijini jana Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa, alisema matukio yanayotokea ni dhahiri kuwa usalama wa wananchi kwa sasa ni mdogo kwa kuwa askari wanaouawa ni watu wenye uzoefu na weledi mkubwa katika kupambana na wahalifu.
“Ni dhahiri kuwa vitendo vya askari kuuawa kwa sasa vimeshamiri, kama askari wenye silaha kali za moto na mafunzo wanauawa kama ndege na kuku nani atabaki salama, je, hawa wananchi ambao hawana mafunzo yoyote watabaki salama, hii hali ni wazi kuwa usalama wa wananchi hasa wa Pwani upo shakani,” alisema Olengurumwa.
Alibainisha kuwa hofu ya kuuawa inaweza ikachangia utendaji kazi wa askari hao kushuka na hivyo kusababisha madhara zaidi.
“Zisipochukuliwa hatua kali za kiupelelezi na kubaini vichaka vya majambazi, kuna hatari kubwa kwa usalama wa nchi na raia wake, hadi sasa hakuna jitihada zozote zinazofanywa kuhakikisha askari hawaendelei kuuawa,” alisema Olengurumwa.
Alisema wahalifu wanaofanya matukio hasa ya kuua askari na kuwapokonya silaha ambazo hazijulikani wanazipeleka wapi endapo wataamua kuzitumia mitaani zinaweza kusababisha madhara makubwa.
Olengurumwa alisema kuanzia mwaka 2015 matukio ya uvamiizi yamekuwa yakijirudia bila kupatiwa ufumbuzi na hadi sasa yameshasababisha vifo vya askari polisi 30.
“Zaidi ya askari polisi 30 wameuawa na bunduki aina ya SMG 60 za polisi zimepotea ama kuibiwa kutoka katika vituo kumi vya polisi kati ya 2015 mpaka 2017,” alisema Olengerumwa.
Alitoa baadhi ya orodha ya matukio hayo ni pamoja na lilitokea Januari 21, 2015 ambapo majambazi wenye silaha walishambulia Kituo cha Polisi Ikwiriri na kuua maofisa wawili na kuondoka na bunduki mbili ndogo za mashine.
Aliongeza kuwa Februari 2, mwaka huo huo katika Kituo cha Polisi Mngeta, Kilombero mkoani Morogoro, kilishambuliwa na bunduki aina ya SMG moja na magazine na makombora 30 zilichukuliwa.
Alilitaja tukio jingine kuwa ni lile la Februari 4, 2015 ambako ofisa mmoja G.7168 PC Joseph Swai, aliuawa Dodoma akiwa anafuatilia taarifa ya kiongozi wa Serikali za Mitaa ambaye alikuwa ameambatana naye akimpeleka kwa mtu aitwaye Tisi Sirii aliyekuwa akitaka kumuua mtoto wake wa miezi nane.
Olengurumwa aliongeza tukio jingine la mauaji ya askari lilitokea Machi 30, 2015 ambapo majambazi wenye silaha wanaotuhumiwa kuwa magaidi, walivamia katika Kituo cha Polisi cha St. Mathew Sekondari barabara ya Kilwa na kuua maofisa wa polisi wawili na kutokomea kusikojulikana.
Mei 29, 2015 pia ofisa wa polisi wa Kituo cha Polisi Tazara, alishambuliwa na majambazi wenye silaha ambao walichukua bunduki yake na kumwacha na majeraha.
Kwa mujibu wa Olengurumwa, katika tukio jingine Agosti 29, 2016 wakati Kikosi Kazi Maalumu cha Polisi kikiendelea na msako wa kufuatilia majambazi wenye silaha mkoani Pwani, ofisa mmoja wa polisi, ASP Thomas Njuki, aliuawa.
Alisisitiza matukio ya kuuawa kwa askari yanatokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi hao ikiwemo uwepo wa mazingira magumu ya kazi kuanzia makazi, vifaa hadi magari.
Kituo hicho kilitoa wito kwa Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani kulichukulia jambo hilo kwa uzito mkubwa na kufanya uchunguzi ili kuweza kuwabaini wahusika na kuwachukulia hatua kali.
Kauli ya Chadema
Kwa upande wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya askari wa Jeshi la Polisi wanane.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Uenezi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa chama hicho, John Mrema, ilieleza kuwa taarifa hizo si tu kuwa ni za kuogofya bali pia ni za kuhuzunisha na kusikitisha hasa ikizingatiwa kuwa ni miezi michache tu iliyopita tukio la kihalifu kama hilo lilitokea maeneo hayo na Taifa kupoteza askari.
Alisema Chadema inatoa salamu za pole na rambirambi kwa IGP Mangu kwa msiba huo mkubwa ambao si tu kuwa ni pigo kwa Taifa bali ni mwendelezo wa matukio ambayo yanaashiria kuwa usalama wetu uko katika mtikisiko au mashaka makubwa .
“Tunamtaka IGP afanye uchunguzi wa kina na achukue hatua stahiki juu ya matukio yote ambayo yamekuwa yakihatarisha usalama wa raia na mali zao nchini kwa muda mrefu sasa ili yaweze kukomeshwa mara moja, Watanzania hatujazoea matukio ya kihalifu kama yanavyoendelea kutokea nchini mwetu,” alisema Mrema.
Alisisitiza Jeshi la Polisi linatakiwa kujipanga upya ili kuzuia matukio kama haya kutokea ama kwa polisi wenyewe au kwa raia wengine kwa kuwa hilo ni jukumu lao la msingi.
Kauli ya ACT
Chama cha ACT Wazalendo kwa upande wake kimetoa wito kwa Watanzania kushikamana na vyombo vya ulinzi na usalama na kutoa ushirikiano kwao kuhakikisha matendo ya namna hii yanakomeshwa.
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Kamati ya Amani na Usalama wa chama hicho, Mohammed Said Babu, chama hicho kilitoa pole kwa familia za maaskari hao.
“Tunachukulia kitendo hiki kama shambulio dhidi ya Jamhuri na hatua kali na madhubuti zinapaswa kuchukuliwa, mlolongo wa matukio ya namna hii unaonyesha kuwa nchi yetu inapambana na kundi lisilo la kawaida na hivyo weledi wa hali ya juu unatakiwa katika kukabiliana na tishio hili dhidi ya Jamhuri yetu,” alisema Babu. | 3 |
Viongozi hao wakiwa katika eneo la Busia, wamezindua kituo cha Forodha kitakachotumiwa kwa pamoja na nchi zote mbili (OSBP) chenye thamani ya Sh bilioni 1.2, kilichojengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza.Katika mazungumzo yao, pamoja na kukubaliana kuongeza ushirikiano zaidi kwenye maeneo ya mipaka kwa kufungua fursa kwa nchi zote mbili, walionesha wasiwasi kuhusu kutumika vibaya kwa mipaka hiyo na wahamiaji haramu.Rais Museveni, alizungumzia mkakati wake wa kulinda rasilimali zilizopo kwenye ziwa Victoria ambako tayari ameweka kikosi cha askari kulinda mipaka ya ziwa hilo.“Samaki wameanza kuisha kwenye ziwa hili. Niliwaachia polisi na idara ya uvuvi kulinda samaki waliobaki lakini nao wameniangusha. Hivyo nimeamua kutumia jeshi kulinda rasilimali hii. Na tayari nimeambiwa idadi ya samaki imeanza kuongezeka,” alisema Museveni.Rais huyo, alitetea uamuzi wake wa kutumia jeshi kulinda mipaka ya ziwa hilo na visiwa vinavyolizunguka jambo lililolalamikiwa na wavuvi kutoka Kenya.Rais Kenyatta aliwataka wavuvi nchini Kenya kuheshimu sheria kwa kuvua samaki wanostahili badala ya kutumia njia haramu za uvuvi zinazoharibu mazingira na vizazi vya baharini.Marais hao katika hotuba zao walisisitizia nia yao ya kuendeleza ushirikiano wa kimipaka ambapo Rais Uhuru aliitaka Idara ya Uhamiaji Kenya kuhakikisha inawaheshimu raia wote wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kama inavyowaheshimu Wakenya.Alisema kuanzia Machi, mwaka huu, raia wote wa jumuiya hiyo wataingia nchini humu bila zuio lolote au viza. | 5 |
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustin Mahiga amekitaka Chuo cha Diplomasia nchini kutoa mafunzo mtambuka ili kukiwezesha chuo hicho kuzalisha wahitimu wanaoendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.Mahiga aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati wa mahafali ya 28 ya chuo hicho na kuongeza kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa kuwa pia itasaidia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya serikali iliyopo katika utekelezaji wa mpango wa uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo Mwaka 2025.Alisema ili kufikia malengo hayo, chuo hicho kinapaswa kufundisha diplomasi ya uchumi sambamba na uchumi wa viwanda ili kuzalisha wahitimu watakaoisaidia serikali kufikia malengo yake kwa kuwa chuo hicho kipo katika nafasi nzuri zaidi ya kufanya hivyo ikilinganishwa na vyuo vingine nchini.Balozi Mahiga alisema chuo hicho pekee katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kina mchango mkubwa katika kukuza masuala ya kidiplomasia, kwa sasa kinapaswa kuwa mstari wa mbele kuisaidia Serikali kwa kufundisha masomo yatakayoendana na mabadiliko hayo ya kiuchumi.“Naombeni maprofesa, walimu na wakufunzi watafsiri hilo na kuja na mipango itakayosaidia kuzalisha wahitimu watakaokuwa na uwezo wa kupata mitaji lakini wawezekezaji watakaokuja nchini kuwekeza katika maeneo mbalimbali kwa kuwa mambo haya yote yanahitaji diplomasia,” alisema Balozi Mahiga.Aliwataka wahitimu pia kutumia elimu waliyoipata kuwatafuta na kuwashawishi wawekezaji wa mataifa mengine, lakini pia kutambua heshima iliyonayo Taifa katika utatuzi wa migogoro mbalimbali na kuitumia nafasi hiyo kuilinda na kuiendeleza.Kwa upande wake, Mkuu Chuo cha Diplomasia, Dk Bernard Achiula alisema katika kuhakikisha chuo hicho kinaenda sanjari na mipango ya serikali kinatarajia, katika mwaka ujao wa masomo kitaongeza udahili wa wanafunzi hatua ambayo pamoja na mambo mengine kitasaidia kuzalisha wahitimu wa kutosha katika soko.Alisema hatua hiyo inatokana na mipango ya serikali ya kukiboresha chuo hicho baada ya kukipatia fedha za ujenzi wa majengo mbalimbali kiasi cha Sh bilioni mbili, jambo litakalosaidia kuongeza nafasi ya udahili kwa wanafunzi chuoni hapo.Aidha alisema katika kutimiza majukumu yake ya utoaji elimu, chuo hicho kimekuwa kikitoa mafunzo mbalimbali yakiwemo ya ushauri wa kitaalam, pamoja na elimu ya mahusiano, hatua iliyokifanya kizidi kujizolea sifa mbalimbali ndani na nje ya taifa.Naye Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Balozi Ombeni Sefue, pamoja na kuipongeza serikali kwa juhudi mbalimbali inazozifanya kukiboresha chuo hicho, alisema matarajio ya mbeleni kwa chuo hicho ni kuzalisha wahitimu watakaoleta tija kwa taifa.Alisema katika kufikia malengo ya serikali ya kuzalisha wataalam hao, chuo hicho kimeendelea kujikita katika mipango mikakati mbalimbali yenye lengo la kuendana na kasi ya mabadiliko ya serikali ya awamu ya tano ili kuliletea maendeleo taifa. | 3 |
NCHI Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na nchi za Bara la Afrika kwa ujumla hazitafi kia mageuzi ya kiuchumi kupitia mapinduzi ya viwanda kama zitaendelea kuwa tegemezi kwa nchi za Ulaya, Amerika na Asia. Hayo yalibainishwa na Rais John Magufuli wakati akifungua Wiki ya Maonesho ya Nne ya Viwanda ya SADC jijini Dar e s Salaam jana. Katika hotuba yake Rais Magufuli alisisitiza ushirikiano miongoni mwa nchi wanachama katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo ili kuwa na mageuzi ya kweli ya kiuchumi. Rais Magufuli alisema sekta ya viwanda ni muhimu katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa nchi wanachama wa SADC na Afrika kwa ujumla kwa kuwa ndiyo inayoweza kusaidia katika kupambana na umaskini.Aidha alisema sekta hiyo itapunguza tatizo la ajira pamoja na kuleta utajiri kama ilivyo kwa nchi za Marekani, Japan, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa na nchi zingine kama hizo zenye uchumi mkubwa. Alisema katika miaka ya 1960 na 1970, uchumi wa nchi za Asia ikiwemo China, India, Korea Kusini, Malaysia, Thailanda na Vietnam ulikuwa ukifanana na uchumi wa nchi nyingi za Afrika, lakini nchi hizo za Asia ziliamua kuchukua hatua mahususi kuleta mageuzi ya viwanda na ndiyo maana leo wamefikia walipo, hivyo nchi za SADC na Afrika yote zinapaswa kutambua kuwa hakuna njia ya mkato ya kufikia mageuzi ya kichumi pasipo kukumbatia mapinduzi ya uchumi wa viwanda.“Mchango wa sekta ya viwanda katika uchumi kwa Afrika kwa Pato la Taifa ni asilimia 10 tu na kwa nchi za Jumuiya ya SADC ni asilimia 11, wakati mchango wa bidhaa za viwandani katika uchumi wa Afrika ni chini ya asilimia 3 kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), lakini kutokana na kutokuwepo kwa uchumi wa viwanda, nchi za Afrika zimeendelea kuwa maskini na kubaki kuwa wazalishaji wa malighafi kwa viwanda vya mataifa ya nje,”alieleza Rais Magufuli. Alisema asilimia 62 ya mauzo ya nje kutoka Afrika ni malighafi ambazo bei yake ni ndogo kwa kuwa wanaopanga bei hizo ni wanunuzi wa nje, lakini kutokana na hali hiyo, nchi za Afrika zimegeuka kuwa wanunuzi wakubwa wa bidhaa kutoka nje kwa gharama kubwa. Katika kuonesha namna gani Jumuiya ya SADC na nchi zingine za Afrika zinavyoathirika kiuchumi kama hazitachukua hatua madhubuti ya kujitegemea kwa kushirikiana, Magufuli alisema thamani ya biashara iliyofanyika kati ya Afrika na Umoja wa Ulaya ilikuwa ni Euro bilioni 280 na kati ya kiwango hicho, Afrika ilinunua bidhaa zenye thamani ya Euro bilioni 149 kutoka Umoja wa Ulaya, lakini ikauza katika Umoja wa Ulaya bidhaa zenye thamani ya Euro bilioni 131.Aliongeza kuwa asilimia 60 ya bidhaa hizo zilizouzwa Umoja wa Ulaya zilikuwa bidhaa ghafi na kutolea mfano uwiano usio sawa wa kibiashara kati ya pande hizo mbili, kwa kusema kuwa kilo moja ya kahawa ghafi kutoka Afrika inauzwa kati ya Dola 1.5 hadi Dola 3 za Marekani lakini kahawa hiyo ikishasindikwa inauzwa kwa Dola kati ya 10-15 za Marekani kwa kilo.“Kukosekana kwa viwanda, biashara kati ya nchi za Afrika imeendelea kuwa chini ya asilimia 20 wakati Latin America asilimia 30, Asia asilimia 40, Ulaya zaidi ya asilimia 60 na nchi za SADC ni asilimia 22,”alisema Rais Magufuli. \Namna ya kujikwamua Baada ya kuonesha namna gani uchumi wa viwanda wa nchi za SADC na Afrika unavyoshindwa kukua ikilinganishwa na mabara mengine, Magufuli alisema njia pekee ya kujikwamua kutoka hapo ni nchi hizo za SADC na Afrika kuamua kufanya mapinduzi ya lazima ya viwanda ili kufikia mageuzi makubwa ya kiuchumi.Alisema uanzishwaji wa wiki ya maonesho ya viwanda ya SADC ni utaratibu mzuri kuelekea mapinduzi ya uchumi wa viwanda kwa kuzingatia mkakati wa kukuza viwanda wa SADC wa mwaka 2015- 2063 ambao pamoja na mambo mengine unasisitiza umuhimu wa kukuza maendeleo, ushindani wa bidhaa na mtangamano kati ya nchi wanachama. Magufuli alizitaka nchi wanachama wa SADC na Afrika kuweka kipaumbele cha kukuza teknolojia miongoni mwao badala ya kufikiria kwenda nchi za mbali, kuuziana malighafi na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa katika SADC na Afrika, kukuza na kuongeza ubunifu kwa vijana ambao ni nguvu kazi katika masuala ya sayansi na teknolojia.Alisema kwa kuwa Jumuiya ya SADC ina watu zaidi ya milioni 300, ni soko kubwa na muhimu kama nchi wanachama wataamua kushirikiana kibishara badala ya kutegemea nchi za Ulaya, Amerika na Asia.Alisema vijana wengi ambao ni nguvu kazi ya Afrika wamekuwa wakimbilia nchi za nje kutafuta ajira, lakini nguvu kazi hiyo ikitumika vizuri italeta mageuzi makubwa ya kiuchumi Afrika.Kwa mujibu wa Rais Magufuli, sekta binafsi na sekta ya umma hazinabudi kushirikiana katika uanzishwaji wa viwanda, kuweka mazingira wezeshi ya uchumi wa viwanda kama vile ujenzi wa miundombinu ya umeme, barabara, reli, anga na bandari, kuondoa vikwazo vya kibiashara ikiwemo kodi, udhibiti na kutaka majadiliano yote yatakayofanyika katika wiki ya maonesho ya viwanda ya SADC kufanyika kwa uwazi kwa manufaa ya Jumuiya nzima. Alisema katika kipindi hiki cha uongozi wake, Tanzania imefanikiwa kujenga viwanda vipya 4,000 vinavyozalisha bidhaa mbalimbali. Katibu Mtendaji SADC Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa SADC, Dk Stergomena Tax, alisema kuwa wiki ya maonesho ya viwanda ya SADC yanayofanyika kila mwaka yanasaidia kuzileta sekta binafsi pamoja na kujenga ushirikiano wa kufanya biashara pamoja nje ya mipaka ya nchi zao.Dk Tax aa lizitaka nchi wanachama wa SADC kutumia fursa za kibiashara zinazopatikana katika eneo huru la biashara la SADAC (SADC Free Trade Area) ambalo ni soko mtangamano la nchi 16 wanachama lenye idadi ya watu milioni 327 ambapo katika mwaka 2016 Pato la Taifa la pamoja lilikuwa Dola za Marekani milioni 599. Waziri wa Viwanda Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema kuwa jumla ya washiriki 3,001 kutoka nchi za SADC ikiwemo Tanzania wanashiriki katika maonesho hjayo yanayoambatana na midahalo mbalimbali. Alisema kati ya waoneshaji 1,576, waoneshaji 1,404 ni Watanzania na waoneshaji 172 ni kutoka nje ya Tanzania. Alisema Ijumaa ya wiki hii wageni watapata fursa ya kutembelea viwanda 20 ambapo viwanda 14 kati ya hivyo vipo Tanzania Bara na viwanda sita viko Zanzibar. Naye Waziri wa Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Amina Salum Ali, alisema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye miundombinu bora barani Afrika ikiwemo reli ya kisasa (SGR) na barabara ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa Viwanda. Alisema kupitia wiki ya maonesho ya nne ya viwanda ya SADC, nchi wanachama watapata fursa ya kuona maendeleo ya viwanda na maendeleo kwa ujumla wake ambayo Tanzania imeyafikia. Mwenyekiti Sekta binafsi Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Salum Shamte, alisema maonesho hayo ni muhimu kwa sekta hiyo kwa kuwa takwimu zinaonesha kuwa asilimia 90 ya ajira ndani ya SADC zinatokana na sekta binafsi. | 3 |
MVUA iliyonyesha jana katika baadhi ya mikoa iliitikisa Dar es Salaam kwa kuvuruga usafiri huku baadhi ya maeneo ya mabondeni wakazi wake wakihaha kutokana na maji kuongezeka kwa kasi kwa muda mfupi Mvua hiyo ilifikia milimita 42.0 wakati Dodoma ikiwa ni milimita 42.7, Kanda ya Ziwa Victoria, Mkoa wa Musoma ikiwa ni milimita 23.1 na Mwanza milimita 22.5.Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kuwa mvua hiyo ni mwendelezo wa mvua za masika zilizoanza kunyesha tangu wiki ya mwisho ya mwezi Februari mwaka huu.Meneja Kituo Kikuu cha Utabiri kutoka Mamlaka hiyo, Samwel Mbuya alisema kuwa kiwango cha juu cha mvua hiyo kilifikia milimita 42.7.Mbuya alisema kuwa ukanda wa pwani katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Pwani na Lindi, mikoa ya kati ikiwemo Dodoma, ukanda wa Ziwa Victoria katika Mikoa ya Musoma na Mwanza pamoja na Mikoa ya Kusini, ndiyo ilipata kiasi kikubwa cha mvua hiyo.“Mvua hii hatuwezi kuiita mvua kubwa kwa sababu mvua kubwa ni ile inayonesha kwa saa 24 na inazidi milimita 50 tofauti na hii ya leo (jana) ambayo imenyesha kwa muda mfupi,” ameeleza Mbuya.Kwa mujibu wa Mtaalamu huyo wa TMA, maeneo ambayo yako kwenye tahadhari ya kupata mvua kubwa katika msimu huu ni pamoja na Ukanda wote wa Pwani, Mikoa ya Lindi na Mtwara, ukanda wa kusini-magharibi katika Mikoa ya Njombe, Mbeya na Rukwa, ukanda wa kati na ukanda wa Ziwa Victoria.Kutokana na mvua hiyo, HabariLeo lilishuhudia baadhi ya miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam ikishindwa kuhimili kiwango kikubwa cha maji ya mvua hiyo.Baadhi ya maeneo hayo ni Tandale kwa Mtogole ambapo daraja linalounganisha eneo hilo na Tandale kwa Alimau, likiwa limefunikwa kabisa na maji na kusababisha maji hayo kusambaa kwenye majumba ya watu.Daraja hilo kila mwaka husababisha mafuriko kusambaa katika eneo hilo kwa sababu ni dogo na liko chini ikilinganishwa na kiasi kikubwa cha maji kinachopita katika Mto Ng’ombe.Eneo jingine ambalo lilizidiwa na mvua hizo ni bonde la Mkwajuni ambapo maji yalijaa na kupita juu ya barabara.Kwa kuwa barabara hiyo iko chini ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam, Julius Ndyamukama, alisema kuwa wataendelea kufuatilia eneo hilo ili kuona kama maji yatakuwa yakipita juu ya barabara kila wakati kama ilivyo Jangwani au la.Ndyamukama alisema watafuatilia pia ili kujua chanzo cha maji hayo kupita juu ya barabara kama vile watu kuvamia kwenye njia ya maji au kama kuna kitu kingine kilichosababisha hali hiyo kutokea.Wakati huo huo, Kampuni inayotoa huduma kwenye mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (UDART), ililazimika kuyaondoa mabasi yake kutoka katika kituo kikuu cha mabasi hayo kilichopo Jangwani jijini Dar es Salaam na kuyapeleka katika vituo vingine vikubwa.Hatua hiyo ya Udart imlielezwa kuwa ni tahadhari ya kuyaepusha mabasi hayo yasipate madhara kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kwa takribani saa tano kuanzia alfajiri jana.Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa Udart, Deusdedit Bugama, amesema, baadhi ya mabasi hayo yamepelekwa kwenye kituo cha Kivukoni kilichopo Posta, Gerezani, Kariakoo na Kimara.Bugama alisema ingawa mvu hiyo haikuathiri shughuli za uendeshaji wa mabasi hayo jana, lakini waliona ni vyema wachukue tahadhari hiyo kabla hali haijawa mbaya.“Barabara haijafungwa kwa sababu maji hayakupita juu ya barabara na huduma ya usafirishaji wa abiria inaendelea; kiasi kidogo cha maji kiliingia kwenye kituo kikuu cha maegesho Jangwani ndiyo maana tumeamua kuyaondoa kwa tahadhari,” alieleza Bugama. | 3 |
['Japo wenyewe hawasemi, ama yawezekana hawataki kunukuliwa wakisema, miaka 30 ya kushindwa kuchukua taji la Ligi ya Primia kwa Liverpool hatimaye inaelekea kufika kikomo. ', 'Hawawezi kusema hadharani, ama kuonesha furaha yao kwa sasa, kwa kuwa katika miaka hiyo 30 kumekuwa na vipindi ambavyo walikaribia kunyakua kombe lakini likawaponyoka.', 'Lakini yaonekana mwaka huu hadithi ni tofauti, ubora wa kikosi ni wa hali ya juu, yawezekana ikawa sahihi kusema kikosi hiki cha sasa ndiyo bora zaidi kuliko vyote katika miongo mitatu iliyopita. ', "Nuru ya ushindi iling'ara zaidi kwa vijana hao wanaonolewa na Mjerumani Jurgen Klopp baada ya kuichapa Leicester City inayoshika nafasi ya pili kwa goli 4-0 siku ya Boxing Day. ", 'Ushindi wa Liverpool uliambatana na kiwango safi cha umiliki wa kandanda, Leicester ambayo watu walikuwa wakiipigia chapuo la kuizuia Liverpool na kufanya maajabu ya kuchukua ubingwa kama mwaka 2016 walikuwa zaidi ya wanyonge katika mchezo huo uliopigwa dimbani kwao. ', 'Kwa matokeo hayo, Liverpool ikafikisha alama 52, na kuifanya ikae kwenye usukani wa ligi kwa tofauti ya alama 13 dhidi ya Leicester yenye alama 39. ', 'Ijumaa Disemba 27, ikawa siku njema pia kwa Liverpool japo hawakushuka dimbani, mabingwa watetezi Manchester City ambao wapo nafasi ya tatu wakapoteza mchezo wao dhidi ya Wolves kwa goli 3-2.', 'Kwa matokeo hayo, pengo baina ya Livepool na Man City yenye alama 38 ni pointi 14. ', 'Ikumbukwe pia kuwa Livepool ana mchezo mmoja mkononi hivyo endapo ataushinda mchezo huo atakuwa na alama 55. ', 'Baada ya mchezo dhidi ya Wolves, kocha wa Man City Pep Guardiola alikiri kuwa safari ya ubingwa kwao imefikia tamati.', '"Pengo ni kubwa sana...ni kitu kisicho na uhalisia kwa sisi kuanza kuwafikiria Liverpool. Kwa sasa tunawapigia hesabu Leicester, tunaamini tunaweza kurudi katika nafasi ya pili," amesema Guardiola. ', 'Kwa upande wa kocha wa Leicester, Brendan Rodgers pia itakuwa ni vigumu sana kuwazuia Liverpool. ', '"(Liverpool) Ni timu nzuri sana. Kiwango chao cha kujiamini kipo juu. Wamekuwa ni wazoefu wa kushinda na hawajapoteza michezo mingi katika miezi 18 iliyopita. Sasa wana wachezaji wa kutosha, uzoefu na ubora wa kuwafanya wamalize kazi mapema." ', 'Kocha wa Liverpool kwa upande wake anaonekana kukagua kila neno analoliongea kuhusu mustakabali wa ubingwa. ', 'Naam, uhalisia ni kuwa bado kuna mechi 20 zinawasubiri kabla ya kumaliza msimu huu. ', 'Nusu yao ya ligi, sawa na michezo 19 itakuwa kesho dhidi ya Wolves. Mpaka sasa Liverpool wameshinda mechi 17 na kutoka sare mchezo mmoja tu dhidi ya mahasimu wao Man United. ', ' "Bado hakuna chochote kilichoamuliwa, sisikii maamuzi yeyote kwenye masikio yangu. Sisi tunajitahidi kufanya kila tuliwezalo kujiandaa na mechi zetu zinazofuata," anadai Klopp. ', 'Licha ya kauli hiyo ya Klopp, uhalisia ni kuwapengo baina yao na timu zinazowafukuza katika msimamo wa ligi ni kubwa.', 'Si jambo linaloyumkinika kuona Liverpool ambayo haijafungwa michezo ya ligi 34 iliyopita kudondosha alama 14 mpaka msimu utakapokamilika mwakani. ', 'Toka mwaka 2019 uanze Livepool imefungwa mchezo mmoja tu wa ligi. ', 'Ili ubingwa uwaponyoke msimu huu, basi watalazimika kufungwa michezo mitano kati ya 20 ijayo, huku wapinzani wao wa karibu, Man City na Leicester washinde michezo yao yote. Hakika hizo zitakuwa hesabu ngumu kutimia.', 'Mpaka sasa Man City washapoteza mechi tano kati ya 19 (mzunguko wa kwanza wa ligi). Msimu uliopita walipoteza mechi nne katika mechi zote 38. ', "Uongozi huu wa ligi wa Liverpool, kwa alam nyingi kama hizo kufikia siku ya 'Boxing Day' mara ya mwisho ulishikiliwa na Manchester United miaka 26 iliyopita msimu wa 1993-1994, ambapo United walinyakua ubingwa. ", 'Kwa namna yeyote ile, Liverpool ni bingwa mteule wa ligi ya Primia msimu wa 2019/2020. ', 'Mara yao ya mwisho kuchua taji hilo ilikuwa ni miaka 30 kamili iliyopita, msimu wa 1989/1990. '] | 4 |
KAMPALA, UGANDA ALIYEKUWA mgombea urais wa Chama cha Forum for Democratic Change (FDC), Dk. Kizza Besigye, amewaambia wafuasi wake kuwa Rais Yoweri Museveni anatumia kodi zao kuwahonga wapigakura. Akimpigia kampeni mgombea wa FDC, Robert Onega, kuwania ubunge katika uchaguzi mdogo wa Manispaa ya Nebbi, Besigye alidai umasikini na ukosefu wa ajira umesababishwa makusudi na vitu vinavyopandikizwa na Serikali ya NRM ili kuwakatisha wananchi tamaa. “Mabilioni ya fedha za walipakodi yanatolewa kwa watu kama rushwa ili kuwapigia kura wagombea wa NRM, huku barabara na hospitali zetu zikihitaji sana fedha hizo kuziboresha,” alidai. Kwa mujibu wa Besigye, Uganda ilikuwa nchi tajiri kabla ya NRM kuingia madarakani mwaka 1986, lakini sasa kila kitu kinaibwa na Serikali ya NRM na kuiacha nchi nzima masikini. Shughuli za biashara zilikwama kwa saa moja wakati maelfu ya wafuasi walipojitokeza katika msafara wa kumpokea Besigye na timu yake kwenye Bustani ya Meya wa Nebbi, ambako mkutano wa hadhara wa Onega ulifanyika. Rais wa FDC, Patrick Amuriat, aliwataka wapigakura wa Nebbi kumpiga kura mgombea bora, ambaye atafanya kazi bila kuchoka kuleta mabadiliko katika eneo lao. Alisema vyama vya upinzani ni sauti ya jamii zisizosikika na hivyo zipewe mamlaka kwa sababu wana uwezo wa kuleta mabadiliko haraka nchini. Kwa upande wake, Onega aliwataka wafuasi wake kuwa watulivu na kuepuka siasa za utengano, ukabila na machafuko. Aliongeza kuwa amelenga kuwaunganisha wapigakura wa Manispaa ya Nebbi kufanya kazi kama timu moja ili kuchochea maendeleo. | 2 |
VERONICA ROMWALD -DAR ES SALAAM KUIMARIKA kwa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo
katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kumewezesha wagonjwa wote
kutibiwa nchini na hakuna aliyepewa rufaa kwenda kutibiwa nje ya nchi. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam juzi na Mkurugenzi wa
Idara ya Magonjwa ya Moyo wa JKCI ambaye pia ni Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dk.
Peter Kisenge. Alisema hayo ni mafanikio makubwa kwa taasisi hiyo kwa
sababu imesaidia kuokoa fedha nyingi za Serikali ambazo hutumika kugharamia
matibabu kwa wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi. Dk. Kisenge alisema mafanikio hayo yamefikiwa kutokana na
uwekezaji mkubwa uliofanywa katika taasisi, hasa kuwekewa vifaa vya kutosha vya
kisasa vinavyohitajika kwa matibabu ya moyo pamoja na wataalamu. “Wagonjwa waliokuwa wakipelekwa nje ya nchi kwa matibabu
kwa gharama za Serikali wamekuwa wakipungua mwaka hadi mwaka tangu kuanzishwa
kwa taasisi hii,” alisema. Pia alisema kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 wagonjwa wa
moyo waliopelekwa nje ya nchi walikuwa 17 tu na kila mmoja aliigharimu Serikali
zaidi ya Sh milioni 30 za matibabu. Alisema kwa sasa taasisi hiyo imekuwa na jina kubwa
kutokana na matibabu ya kibingwa yanatolewa na wamekuwa wakitibu wagonjwa wa
ndani na nje ya nchi. “Tunaaminika Afrika, hasa ukanda wa Mashariki na Kati,
tunapokea wagonjwa kutoka nje ya nchi, hii ina maana kwamba wana imani na
huduma zinazotolewa. “Jana (juzi) tu
nimemuona mgonjwa kutoka Misri, hata kama hakutoka huko kuja hapa nchini kwa
matibabu, pengine ameugua akiwa hapa, hii inatupa picha kwamba hayo mataifa
yana imani na sisi,” alisema. Alisema taasisi hiyo hivi sasa inapokea wagonjwa wa nje
(out patients) 300 kwa siku, wagonjwa 10 hadi 15 ni wa rufaa na wagonjwa wawili
kati ya hao ni kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati. Pia alisema JKCI inatoa mafunzo kwa madaktari mbalimbali na
kwa mwaka madaktari wapatao 20 wanapata mafunzo katika taasisi hiyo. Dk. Kisenge alisema hakuna mgonjwa anayefika na asipatiwe
huduma, na wagonjwa wote wanatibiwa bila kujali hali zao kifedha. “Gharama zetu ni za
kawaida, lakini hakuna mgonjwa atakosa huduma, tuna wale ambao hawawezi
kugharamia matibabu, lakini nao tunawahudumia,” alisema. | 0 |
['Mwanariadha wa Kenya Conselsius Kipruto alimshinda Lamecha Girma wa Ethiopia katika fainali ya kusisimua ya mbio za mita 3,000 kuruka vizuizi na maji katika mashindano ya Dunia ya riadha yanayondelea mjini Doha Qatar.', 'Girma aliongoza mbio hizo hadi sekunde ya mwisho lakini Kipruto, ambaye alionekana kama alifanikiwa kumfikia na na kunyakua ushindi uliosaidia kuhifadhi taji la dunia la mbio hizo.', 'Alifahamu ushindi wake sekunde 30 baada ya wasimamizi wa mashindani hayo kuthibitisha ushindi wake.', 'Kipruto, 24, alikimbia mbio hizo kwa muda wa dakika 8:01.35. ', 'Mwanariadha huyo wa miaka 18 wa Ethiopia aliweka rekodi mpya ya kitaifa ya mbio hizo kwa muda wa dakika 8:01.36.', 'Mwanariadha wa Morocco Soufiane el Bakkali aliibuka wa tatu kwa kumaliza mbio hizo kwa 8:03.76.', 'Akizungumza baada ya mashindano hayo, Kipruto, alielezea mita 100 ya mwisho kama muda \'\'wa kushangaza zaidi...Si kuamini macho yangu".', 'Akizungumzia muda wakusubiri matokeo rasmi aliesma: "Nilikua naomba: \'wacha mshindi awe ni mimi.\'"', 'Kenya imetawala mbio hizi tangu mwaka wa 1991 Moses Kiptanui aliposhinda dhahabu katika mbio za dunia mjini Tokyo na kuhifadhi ubingwa huo mwaka wa 1993 na 1995.', 'Kwa Jumla Kenya imeshinda mbio hizo mara 12 kwenye mashindano ya dunia.', 'Majirani wa Kenya, Ethiopia wamekua wapinzani wao wakuu katika mashindano ya riadha, huku mataifa hayo mawili yakitawala mbio za masafa ya kadri na ya masafa marefu.', 'Ushindi wa Kipruto unamaanisha kuwa Kenya imejinyakulia medali tatu za dhahabu katika mashindano hayo ya Dunia ya Riadha wakilinganishwa na mahasimu wao Ethiopia walio na medali moja ya dhahabu.'] | 4 |
SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli imevunja rekodi kwa kuunganishia umeme wananchi 949,000 kwa kipindi cha miaka mitatu, ikilinganishwa na idadi ya wananchi milioni 1.3 waliounganishiwa huduma hiyo miaka 50 iliyopita baada ya Uhuru. Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, alipokuwa akizindua uwashaji umeme kwenye kitongoji cha Kisasa, kata ya Tambani, wilaya ya Mkuranga na kueleza kuwa, lengo ni kuhakikisha umeme unamfikia kila mwananchi. Alisema idadi hiyo imefikiwa kupitia miradi mbalimbali ya umeme ikiwamo inayosimamiwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA), Ujazilizi na Tanesco, lengo likiwa ni kuwafikia wananchi wote wa Tanzania ifikapo 2021. “Awamu hii ya tano chini ya Rais Magufuli imedhamiria wananchi wote kupata nishati ya umeme kwani umeme ni maendeleo na kwa miradi mingi ambayo inaendelea malengo ya nchi nzima yatafikiwa ifikapo 2021,” alisema Mgalu. Alisema mradi wa umeme katika miji iliyo pembezoni ambao utawafikia wananchi 4,293 wa awali, Tanesco imetenga kiasi cha Sh bilioni 3.3 kwa mwaka wa fedha 2019/2020. “Mradi huu utavifikia vijiji 11 na vitongoji 30, ambapo REA Awamu ya Tatu mzunguko wa pili utaanza Desemba, mwaka huu na mradi wa Ujazilizi awamu ya pili utahusisha mikoa tisa,” alisema. Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uvuvi na Mifugo na Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdala Ulega, alisema wakati anaingia kwenye nafasi hiyo umeme ulikuwa katika vijiji visivyozidi 10, lakini kwa sasa vimefika vijiji 43. Alisema licha ya vijiji hivyo kuwa na umeme katika kata za Panzuo, Visegese, Njianne, Kitomondo, Magawa, Bupu na Mchonga, lakini pia mwaka huu huduma hiyo itapelekwa katika vijiji na kata zote. Kwa upande wake, Meneja wa Tanesco Wilaya ya Mkuranga, Octavian Mmuni, alisema umeme uliowekwa kwenye kata ya Tambani una njia kubwa ya kilometa sita na njia ndogo yenye urefu wa kilometa 11 na utawafikia watu 101 ambao wameshalipia. Alisema mradi huo una thamani ya zaidi ya Sh milioni 400 na umefikia asilimia 96. | 3 |
THE
HAGUE, UHOLANZI WAENDESHA Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa
ya Jinai, ICC, wamekubali ombi la kuachiwa huru rais wa zamani wa Ivory Coast,
Laurent Gbagbo, lakini kwa sharti kwamba asirejee katika nchi yake kama
anavyotaka. Kwa mujibu wa Mwendesha Mashitaka Mwandamizi wa Mahakama
hiyo, Helen Brady amewaambia majaji kuwa, wana wasiwasi kwamba huenda Gbabgo na
mpambe wake, Charles Ble Goude wasirejee katika mahakama hiyo iwapo majaji wa
ICC watatoa uamuzi wa kusikilizwa upya kesi zao. Hata hivyo, wakili wa Gbagbo, Emmanuel Altit,
anasisitiza kuwa mteja wake anapaswa kuachiwa huru mara moja bila masharti
yoyote na aruhusiwe kurejea nchini kwake haraka iwezekanavyo. Waendesha Mashitaka wa Mahakama ya ICC ambao walikata
rufaa kupinga uamuzi wa wawili hao kuachiwa huru, wanataka waachiwe huru na
kisha wapelekwa katika nchi jirani na Uholanzi, sambamba na kutwaliwa pasi zao
za kusafiria. Mwezi uliopita, ICC ilifuta mashtaka na kuwaachilia huru Gbabgo pamoja na mpambe
wake, Charles Ble Goude, ambao walikuwa wanakabiliwa na tuhuma za kuhusika
katika ghasia baada ya uchaguzi katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi. Wawili hao walikuwa wanakabiliwa na mashtaka ya jinai
dhidi ya binadamu katika mwaka 2010 na 2011 katika vita ya ndani nchini mwao
ambako watu 3,000 waliuawa. | 2 |
JUMLA ya miradi 39 yenye thamani ya Sh bilioni 16.09 iliyotekelezwa katika halmashauri nane za mkoa wa Tabora inatarajiwa kuzinduliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru unaowasili mkoani humo leo.Hayo yalisemwa jana na mkuu wa mkoa huo, Agrey Mwanri, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya ujio wa Mwenge huo.Alisema miradi itakayozinduliwa ni sehemu tu ya miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa katika halmashauri zote nane za mkoa huo.Mwanri alisema Mwenge ukiwa mkoani humo utakimbizwa katika halmashauri zote na utaweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.“Mbio za Mwenge zitaambatana na maonesho ya shughuli mbalimbali za uzalishaji mali, bidhaa za vikundi vya vijana, akinamama na watu wenye ulemavu ambao ni wajasiriamali katika kila halmashauri,” alisema.Alisema pia kutakuwa na maonesho ya shughuli za sekta ya afya, maji na mikesha itakayohusisha shughuli za upimaji virusi vya ukimwi (VVU), malaria na magonjwa mengineyo, hivyo akawataka wananchi wajitokeze kwa wingi.Mkuu huyo wa mkoa alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa leo asubuhi wilayani Igunga ukitokea mkoa wa Singida na utapitia miradi mbalimbali kabla ya kukabidhiwa kwa halmashauri ya Nzega Mji kesho.Alisema keshokutwa utaingia Nzega DC, Agosti 29 Uyui DC, Agosti 30 Kaliua DC, Agosti 31 Urambo DC, Septemba Mosi, Tabora manispaa na Septemba 2 utakuwa, Sikonge ambapo kesho yake utakabidhiwa kwa mkuu wa mkoa wa Mbeya.Alitaja kauli mbiu ya mbio hizo kuwa ni ‘Maji ni haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa’, huku kukiwa na kaliu mbiu nyingine ndogo zinazohusu ukimwi, malaria, rushwa na dawa za kulevya. | 3 |
Mwadui inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Simba Jumamosi hii katika mchezo wa Ligi Kuu utakaochezwa kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga. Mwadui FC iko nyuma ya Simba kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 21 zikitofautiana kwa pointi mbili hivyo kila moja itapambana kuhakikisha inashinda na kumpita mwenzake.Akizungumza na gazeti hili jana, Julio aliwahi kuwa kocha wa Simba mara kadhaa kwa nyakati tofauti alisema kikosi chake kimejipanga kutoa kichapo kwa Simba ili kuendelea kujisogeza katika nafasi ya kulisogelea taji la ubingwa wa ligi.“Tutawaonyesha Simba kazi, nashukuru nina kikosi kizuri kina wachezaji wazoefu ambao wamekuwa wakipambana, naamini Simba haitaondoka salama katika mchezo huo,” alisema. Timu hiyo imetoka kufanya vizuri katika michezo miwili iliyopita ambapo iliifunga Stand United mabao 2-0, na kuifunga Ndanda FC mabao 2-1.Wakati timu hiyo ikifanya vizuri kwenye uwanja wake wa nyumbani, Simba imetoka kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Toto Afican ya Mwanza. Huo ni mchezo wa pili kwa Simba baada ya mwingine uliopita pia kulazimishwa sare dhidi ya Azam FC kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. | 4 |
['Manchester United wameweka wazi kuwa kumsajili mshambuliaji ni kipaumbele katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari na wameelekeza macho yao kwa mshambuliaji wao wa zamani Zlatan Ibrahimovic, 38. (Daily Express)', 'Timu hiyo ya Old Trafford pia inampa nafasi ya juu kumsajili kiungo wa West Ham Declan Rice 20, ifikapo Januari, lakini huenda ikawagharimu pauni milioni 80. (Goal via Mail)', 'Kocha wa Crystal Palace, Roy Hodgson, 72, yuko kwenye mazunguzo kuhusu mkataba mpya. (Sky Sports)', 'Wolves wanamtolea macho mchezaji wa nafasi ya ulinzi Gabriel Magalhaes wakati huu wakiwa na nia ya kumtafuta mchezaji wa nafasi ya ulinzi mbadala wa machezaji aliyejeruhiwa Willy Boly.(Daily Mail)', 'Wakala wa mchezaji winga Tahith Chong amewaonya Manchester United kuwa watatazama maombi kutoka sehemu nyingine kama klabu haitawasilisha masharti ya mikataba ya kuridhisha, baada ya mkataba wake kuisha majira ya joto yajayo.(Manchester Evening News)', 'Roma wako tayari kutoa ofa ya pauni 12.9 kwa Manchester United kwa Chris Smalling, 29 baada ya mchezaji huyo wa nafasi ya ulinzi kuanza vyema katika klabu inayocheza ligi ya Serie A. (Guardian)', 'Mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford, 22, huenda akawa amepata jeraha la mguu wakati akishangilia bao lake lililotokana na mpira wa adhabu dhidi ya Chelsea katika michuano ya kombe la EFL.(Mail)', "Liverpool imetakiwa kumshawishi nyota wa Chelsea N'Golo Kante,28. (Racing Post, via Mirror)", 'Newcastle United itafanya mkutano kuhusu usajili wa mchezaji juma lijalo. (Newcastle Chronicle)', 'Meneja wa Derby County Phillip Cocu amethibitisha kuwa mchezaji wa timu ya taifa ya England Wayne Rooney,34, amekuwa kwenye viwanja vya mazoezi vya klabu hiyo. (Derby County)', 'Vilabu vitatu vinataka kumsajili kiungo wa pembeni wa Juventus Emre Can, 25, katika msimu wa dirisha la usajili mwezi Januari.(Calciomercato)', "Meneja wa Saint Etienne Claude Puel amekosoa uamuzi wa klabu kumuuza mchezaji wa nafasi ya ulinzi William Saliba,18, kwenda Arsenal, akisema mpango huo ni wa ''muda mfupi'' . (Metro)", 'Wakala wa Sassuolo , Stefano Sensi amekuwepo Barcelona, na kumfanya kuhusishwa na tetesi kuwa mchezaji huyo atajiunga na mabingwa wa Uhispania. mchezaji huyo anaichezea Inter Milan kwa mkopo. (Sport - in Spanish)', 'Nantes inataka kumsajili mchezaji wa zamani wa Newcastle Hatem Ben Arfa. Mchezaji huyo wa miaka 32 yupo kwa uhamisho wa bure. (RMC Sport - in French)'] | 4 |
SAKATA la malumbano makali yaliyodumu kwa zaidi ya wiki mbili baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kudai Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad, amelidhalilisha Bunge kwa kuliita dhaifu, limechukua sura mpya baada ya CAG kukubali kuitikia mwito huo wa Spika.Katika hatua nyingine, Spika Ndugai amepuuza madai kuwa amevunja Kamati mbili za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zinazofanya kazi kwa ushirikiano na CAG.Amefafanua kuwa kilichotokea ni wajumbe wa kamati hizo, kutawanywa kwenye kamati zingine wakati huu ambao hawana kazi ya kufanya. Januari 7 mwaka huu, Spika Ndugai alivieleza vyombo vya habari jijini Dodoma kuwa CAG na Mbunge wa Kawe jijini Dar e s Salaam, Halima Mdee ambaye aliunga mkono kauli ya CAG kuwa Bunge ni dhaifu, wanapaswa kufika mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge Januari 21 na 22 ili wahojiwe.Kauli hiyo ya Spika ilizua mjadala mkali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, kwa madai kuwa Spika hana mamlaka kisheria, kumwita na kumhoji CAG kwa kuwa CAG analindwa kikatiba kutoitwa na kutohojiwa na mamlaka au mtu yeyote.Baada ya sakata hilo kudumu kwa zaidi ya wiki mbili sasa, hatimaye CAG Prof Assad alijitokeza jijiini Dar es Salaam jana mbele ya vyombo vya habari na kusema kuwa amepokea mwito huo wa Spika Jumanne ya Januari 15, na kuthibitisha kuwa atakwenda mbele ya Kamati hiyo ya Bunge Januari 21 ili kuhojiwa.CAG alisema kuwa majibu yake aliyoyatoa kwenye mahojiano nje ya nchi kuwa Bunge ni dhaifu, hayakuwa na nia ya kulidhalilisha Bunge. Alisema maneno “udhaifu” na “mapungufu” ni lugha ya kawaida kwa wakaguzi, katika kutoa maoni ya utendaji wa mifumo ya taasisi mbalimbali, japo yanaweza kuchukua tafsiri tofauti kwa watu wengine.“Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni chombo ambacho hakiwezi kufikia ufanisi unaohitajika katika utendaji wake, kama ripoti zake hazitafanyiwa kazi ya kuridhisha na kwa wakati na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Bunge ni taasisi ambazo lazima zielewane na kufanya kazi kwa karibu sana; ninaamini kuwa mpaka sasa nina mahusiano mazuri na yenye tija, si tu kati yangu na Spika, bali na Bunge zima,”alieleza CAG CAG Assad.Alisema uhusiano huo ni muhimu kati ya pande hizo mbili katika kutekeleza majukumu yao ya kikatiba, hivyo hauna budi kuenziwa na kudumishwa. Profesa Assad alisema kuwa ofisi yake, haina namna ya kuathiri tafsiri ya viongozi, wanasiasa na wachangiaji wa kawaida, bali kitu cha muhimu ni uungwana kutawala katika mawasiliano yao.Spika Ndugai akanusha kuvunja kamati Mapema jana asubuhi, Spika Ndugai akiwa na Kamati ya uongozi ya Chama cha Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika, alivieleza vyombo vya habari kuwa katika mfumo wa Jumuiya ya Madola, CAG ni ofisa wa Bunge. Ndugai alisema kwa mantiki hiyo, CAG ambaye ni Ofisa wa Bunge hawezi kumgomea Spika.Alisema CAG anatoka katika Mhimili (Bunge) ambao kazi yake kikatiba ni kuisimamia Serikali, hivyo badala ya wabunge kufanya kazi ya kufuatilia hesabu za Serikali, wanamwajiri CAG kufanya kazi hiyo na baadaye kuwapelekea majibu aliyoyapata.Alisema kwa kuwa Bunge lina wajibu wa kuisimamia serikali, ripoti ya CAG inalisadia Bunge kuishauri na kuielekeza serikali, hivyo sakata hilo kati yake na CAG litakwisha kwa kuwa si jambo kubwa.Kutokana na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT- Wazalendo) kulivalia njuga sakata hilo la Spika na CAG, Spika Ndugai alisema kuwa anapata taabu sana na Zitto kwa kuwa chama chake, kina mbunge mmoja tu, ambaye ni Zitto mwenyewe, hivyo akimfukuza atasababisha chama hicho kukosa uwakilishi bungeni.Spika alisema kuwa Zitto anahangaika na jambo hilo, kwa lengo tu la kupotosha na kujipatia umaarufu. Lakini, alisema uvumilivu utakapomwishia, atachukua hatua dhidi yake.Madai kuwa Spika amezifanyia mabadiliko Kamati za LAAC na PAC, Ndugai alipuuza vikali madai hayo. Alisema baada ya Kamati za Bunge kumaliza shughuli zake ndani ya wiki mbili, wajumbe hao wa LAAC na PAC wataendelea na majukumu yao kama kawaida Bunge litakapoanza.Aidha, Kamati ya Uongozi ya Chama cha Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika, ilikutana jana kwa siku moja jijini Dar es Salaam chini ya Uenyekiti wa Spika wa Kenya, Justin Muturi, kupitisha bajeti ya jumuiya ya hiyo ya mwaka 2020 Kanda ya Afrika. | 3 |
CAPE TOWN -AFRIKA KUSINI MLINZI wa zamani wa Rais Paul Kagame wa Rwanda, Camille Nkurunziza, ameuawa na watu wenye silaha katika Jiji la Cape Town nchini hapa. Nkurunziza ni mtu wa pili mwenye hadhi ya juu kuuawa nchini hapa baada ya mauaji ya aliyekuwa Mkuu wa Ujasusi nchini Rwanda, Kanali Patrick Karegeya mwaka 2014. Waziri wa Nchi wa Rwanda anayeshughulikia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Olivier Nduhungirehe, aliandika kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa Nkurunziza aliuawa na polisi wa hadhi ya juu baada ya kukataa kukamatwa akihusishwa na kitendo cha kuteka gari. Taarifa nyingine zinaeleza kuwa gari hilo analohusishwa Nkurunziza kuteka ni aina ya Toyota Etios. “Hivyo, Camille Nkurunziza, mfuasi wa kundi la kigaidi la RNC la Kayumba Nyamwasa na lile la FLN la Callixte Nsabimana (Sankara), alikuwa pia ni mtekaji nchini Afrika Kusini. Aliuawa jana (juzi) jioni na polisi wa hadhi ya juu wakati alipokataa kukamatwa akiwa na kisu. Unapokuwa mhalifu, ni mhalifu siku zote,” aliandika waziri huyo kupitia Tweeter Ijumaa. Kifo cha Nkurunziza kimekuja siku chache baada ya Meja Callixte Nsabimaana anayefahamika kwa jina jingine la Sankara, kiongozi wa waasi aliyekuwa akituhumiwa kupanga mauaji katika maeneo ya mipaka ya Rwanda kutiwa hatiani kwa kosa la ugaidi na mengine, na aliripotiwa kukiri kufanya kazi na Serikali za mataifa mengine dhidi ya Rwanda. Inaelezwa Nkurunziza baada ya kumgeuka Rais Kagame na kukimbilia uhamishoni nchini Afrika Kusini, huko alikutana na Meja Sankara. Tangu alipokimbilia huko na kukutana na Meja Sankara, inaelezwa alikuwa mkosoaji mkubwa wa Rais Kagame, akimshutumu kuwa hana uvumilivu na maoni yanayompinga. Meja Sankara alikamatwa mwezi uliopita akihusishwa na kundi la National Liberation Front (FLN), akishutumiwa kufanya uasi na zaidi mashambulio ndani ya Rwanda kutoka katika eneo la msitu karibu na Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Aliripotiwa kutiwa hatiani kwa makosa 16, ikiwamo ugaidi na mauaji, na kupewa masharti ya msamaha kwa uhalifu wake. Desemba mwaka jana, Meja Sankara alidai kuwajibika kwenye tukio la kuchoma moto basi la abiria katika msitu wa Nyungwe – eneo ambalo ni maarufu kwa watalii wanaofika kutazama sokwe. Tukio hilo lilisababisha vifo vya watu wawili na wengine wengi wakiwa wamejeruhiwa. Mashambulio hayo yalisababisha nchi za Magharibi zikiwamo Ufaransa, Ujerumani, Canada na Australia kuwashauri raia wake kutotembelea eneo hilo. Ukiacha uhusiano wake wa karibu na Meja Sankara inaelezwa kuwa Nkurunziza pia ni ndugu wa Sajenti Innocent Karisa ambaye alitekwa nchini Uganda mwaka 2013 na kwa sasa yupo jela nchini Rwanda baada ya kutuhumiwa kuwa mfuasi wa kundi pinzani la Rwanda National Congress. Wakati hali ikiwa hivyo, kwa upande mwingine inaelezwa Nkurunziza atakumbukwa kwa kuanzisha kampeni aliyoipa jina la ‘Kipindi cha tatu cha Kagame’, ambayo ilijizoelea umaarufu mkubwa kwa wapinzani nchini Rwanda. Mkuu wa Majeshi wa zamani wa Rwanda, Jenerali Nyamwasa naye pia aliwahi kunusurika majaribio mawili ya kuuawa. Jenerali huyo alikimbilia uhamishoni Johannesburg mwaka 2010 baada ya kile kinachoelezwa kuwa ni kutofautiana na mshirika wake wa zamani, Rais Kagame. Miezi michache baadaye alipigwa risasi mjini Johannesburg, lakini Rwanda ilikanusha kuhusika na shambulio hilo ambalo alipona. Kundi alilomo Sankara la FLN linaloendesha harakati zake za kudai mabadiliko ya kidemokrasia likiwa na silaha, ni kundi la upinzani lililoanzishwa na Paul Rusesabagina, hotelia ambaye matendo yake wakati wa mauaji ya halaiki nchini Rwanda mwaka 1994 yalichezewa filamu huko Hollywood ikipewa jina la ‘Hotel Rwanda’. | 3 |
KUNA maudhi mengi kwenye uhusiano, lakini kubwa zaidi ni ile ya kupotezewa muda kisha kuachwa. Hili huwatokea zaidi wasichana.
Anakuwa na penzi la dhati kwa mwanaume, anawekeza muda na mapenzi yake ya dhati lakini mwisho wa siku, kumbe jamaa hana time naye.
Amemfanya demu wa kuzugia. Wanawake wanapenda kuwajua vizuri wanaume wanaokuwa nao, lakini wanaume ni wajanja sana na wanaweza kujificha wasigundulike kirahisi kinachoendelea kwenye uhusiano wanaokuwepo.
Kujua inasaidia kuchukua hatua. Tatizo ni kwamba wanawake wengi wakipenda, husahau kila kitu. Wao hubaki na jambo moja tu; wanapenda! Mengine hawana time nayo.
Inawezekana kuna mengi ya kufanya ili kumjua mwanaume wako, lakini hapa nimekuandalia dondoo chache.
MWEKEE MITEGO
Kitu muhimu zaidi cha kufanya ili kumjua mwanaume wako ni kumfuatilia kwa karibu. Fanya hivyo kwa kutumia ujanja wa hali ya juu ili asijue kuwa unamtega.
Atafanya mambo yake gizani mpaka lini? Kuna siku utagundua na kumuacha aendelee na umalaya wake kama ameona ndiyo maisha.
Usikubali kabisa kuwa katika penzi la kitumwa, penzi la kisaliti, kuwa na mtu ambaye anakuchanganya wa kazi gani zaidi ya kukupotezea muda na kukukaribishia machozi?
HATAKI UJULIKANE
Hii ni alama nyingine walizonazo matapeli wa mapenzi, ni watu wa kufanya mambo kwa upekee sana. Kila dakika hakaukiwi na neno nakupenda sana, lakini moyoni mwake hakuna alama hata moja ya mapenzi kwako.
Ni vigumu kumtambua mtu wa aina hii lakini chunguza kuhusu hili, hapendi kabisa kukukutanisha na rafiki zake na hata mkikutana nao kwa bahati mbaya basi hatakutambulisha na kama akikutambulisha hatakutambulisha kama mpenzi wake rasmi.
Ataishia kusema ninyi ni marafiki mlioshibana! Tangu lini mpenzi akatambulishwa kama rafiki? Baadaye utakapomuuliza hawezi kuwa na jibu la maana, atabaki kukuambia hata kama akikutambulisha kama rafiki, jamaa ataelewa kuwa ni mpenzi wake, hii inaingia akilini kweli?
Huo ni ulaghai na anaogopa kukutambulisha kama mpenzi maana tayari ameshaonwa akiwa na wapenzi wengine. Jiulize, ikiwa leo hii anashindwa kukutambulisha vyema kwa rafiki zake, vipi kwa ndugu zako?
Ataweza kuwa na ubavu wa kufika kwa wazazi wako na kufuata taratibu zote za ndoa?
MSIRI KUPITILIZA
Hii ni alama nyingine waliyonayo wanaume wa aina ninayoielezea katika mada hii. Siku zote mambo yao ni kwa siri kubwa, kama mna ahadi ya kukutana, hataki muongozane, atakuambia mkutane moja kwa moja sehemu husika.
Hata muda wa kuondoka atafanya kila njia ili kila mmoja aondoke mwenyewe na kama mkiondoka pamoja basi ujue ni usiku na hakuna atakayewaona.
Ikitokea akakubali kuongozana na wewe, hatapenda muongozane pamoja. Atalazimisha utangulie mbele yeye afuate nyuma, kwa nini? Kwa sababu anaogopa kujulikana kuwa yeye ni mpenzi wako.
Fikiria, kama anaogopa, anakupenda kweli? Mapenzi gani hayo yanafanywa kwa siri? Anakupotezea muda huyo. HAPENDI NDUGU WAFAHAMIANE
Mpenzi wa aina hii ni mjanja sana, kwanza kabisa atajifanya mtu mwenye ubize sana, yote hii ni kukwepa kuwajua ndugu zako au wewe kuwajua ndugu zake!
Wakati mwingine anakuwa hapendi ndugu zako na wake wakutane wakijua wazi kuwa nyie mna uhusiano, hili ni tatizo.
Hakuna uhusiano wenye heri na malengo ya kuishi pamoja siku zijazo ukawa wa kificho cha kiasi hicho. Kama ana nia na wewe basi atahakikisha anawafahamu baadhi ya ndugu zako na wewe unawafahamu baadhi ya ndugu zake, hayo ndiyo mapenzi ya kweli.
Mapenzi hayaishii kwa nyie wawili pekee bali hata kwa ndugu zenu. Mnapojuana inakuwa rahisi kusaidiana hata katika mambo mengine ya kawaida.
Lakini kumbuka, jambo hilo haliwezi kuwa la muhimu, wakati mwenzako hana wazo la kukuoa! Wakati ukiwaza maisha, ukiwa na ndoto za kuolewa naye, mwenzako anawaza ngono tu.
Rafiki yangu, mwili wako una thamani kubwa sana, uheshimu. Usijishushe kiasi hicho, ukigundua hayo na mengine yanayofanana na hayo ni bora kuchukua hatua kwa kuangalia ustaraabu mwingine.
Kumbuka huyo anayekupotezea muda na kukuchezea hivi sasa, hana thamani kama aliyeandaliwa kwa ajili yako. Yupo lakini hujakutana naye – ni muda tu.
Je, unapenda kujifunza masomo haya zaidi kupitia group la WhatsApp la Love Moment? Kama ndivyo karibu inbox, andika ujumbe wako ukitaka kujiunga na kundi hilo, nasi tutakuunganisha.
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Saikolojia ya Uhusiano, aliyeandika vitabu kama True Love, Let’s Talk About Love na Maisha ya Ndoa. Kwa sasa anaandaa kitabu chake kipya cha SIRI ZA NDOA YENYE FURAHA kitakachokuwa mitaani hivi karibuni. | 3 |
["Kinyang'anyiro cha kuwania kombe la klabu bingwa duniani kimeanza Jumatano huku kila mechi ikirushwa hewani moja kwa moja katika BBC. ", 'Bingwa wa kila bara na waandaaji wa michuano hiyo Qatar wanakutana katika siku 10 katika mechi za muondoano ili kuamua ni nani ambaye atatawazwa bingwa wa dunia huku Liverpool ikiingia katika nusu fainali ya mashindano hayo. ', 'Je ni kwa nini unafaa kutazama mechi hizo? BBC inakupatia sababu tano.', 'Huenda hakushangaza ulimwengu akiwa Inter Milan , lakini mshambuliaji wa Flamengo Gabriel Barbosa maarufu kama Gabigol ni muhimu kumtazama. ', 'Iwapo ulitazama fainali ya michuano ya mwezi Novemba ya Copa Libertodores katika BBC 2 moja kwa moja utajua inamaanisha nini. ', 'Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ambaye ameshinda mechi tano akiichezea Brazil alifunga magoli mawili katika fainali baada ya Flamengo kutoka goli moja chini na kuishinda River Plate 2-1 na kushinda Copa Libertadores tangu 1981. ', 'Baadaye alipewa kadi nyekundu kwa kuukejeli uamuzi wa refa. ', 'Je iwapo tutakwambia kuna timu moja katika michuano hiyo ilioshiriki katika kombe la Ufaransa msimu huu kutoka katika eneo lililo umbali wa maili 10,000?. ', 'Hienghene Sport ni timu ya pili nje ya Austria ama New Zealand kushinda kombe la ligi ya Oceania na kufuzu katika michuano ya klabu bingwa duniani. ', 'Waliwashinda wenzao wa Caledonia Magenta katika fainali. ', 'Kuhusu ubora wa michuano hiyo , mfungaji wa magoli mengi Ross Allen - ambaye alifunga magoli 11 akiichezea Wellington - kwa sasa anaichezea klabu ya Guensey katika daraja la nane la ligi ya Uingereza. ', 'Eneo la New Caledonia ni eneo la Ufaransa lililo katika eneo la Pacific - ambalo lilipiga kura ya kutokuwa na uhuru katika kura ya maoni mwaka uliopita - limekuwa mwanachama kamili wa Fifa tangu 2004. ', 'Kutokana na hali yao, washindi wa kombe la Caledonia wanafuzu kushiriki katika kombe la Coupe de France, huku Hienghene Sport ikipoteza katika katika awamu ya kwanza 2013, 2015 na mwezi uliopita.', 'Liverpool ina fursa ya kutawazwa mabingwa wa dunia kwa mara ya kwanza.. The Reds licha ya kushinda mataji sita ya Ulaya , hawajashinda fainali ya kombe klabu bora duniani. ', 'Walipoteza taji hilo la International Cup kwa Flamengo mwaka 1981 na baadaye kwa Independente 1984 na kukataa kushiriki 1977 au 1978. ', 'Wameshiriki katika mchuano mmoja wa kombe la klabu bora duniani ikipoteza 1-0 katika fainali kwa Sao Paolo nchini Japan 2005 baada ya kuilaza klabu ya Costa Rica Saprissa 3-0 katika nusu fainali. ', 'Mechi yao ya nusu fainali Alhamisi ijayo- siku moja baada ya timu tofauti ya Liverpool kukabiliana na Aston Villa katika kombe la Carabao nchini Uingereza - inaweza kuwa dhidi ya timu ya Mexico ya Monterrey, ambayo ilishinda ubingwa wa ligi ya Concacaf. ', 'Liverpool baadaye itacheza tena siku ya Jumapili , katika fainali ama kuwania nafasi ya tatu. Kombe la klabu bora duniani limeelekea Ulaya katika misimu yote ya miaka sita iliopita , huku Real Madrid ikishinda fainali tatu zilizopita. ', 'Washindi wake hawafuzu moja kwa moja, hivyobasi Real Madrid hawawezi kutetea taji lao. ', 'Timu ya pekee ya Ulaya kushindwa kushinda taji hilo katika kipindi cha miaka 12 iliopita ni Chelsea mwaka 2012 . Manchester United iliibuka mshindi wa michunao hiyo 2008.', 'Kombe la dunia litachezwa nchini Qatar miaka mitatu kutoka sasa - na pia mwezi Disemba . ', 'Hivyobasi hii ni fursa kuona taifa hilo dogo linaweza kuhimili kuandaa michuano ambapo mashabiki watakuwa wakitoka kutoka kila eneo.'] | 4 |
MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), imeweka mfumo katika mipaka mbalimbali ya nchi ili wafanyabiashara wa nchi za nje wakiwemo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kuzifi kia bidhaa katika mfumo ulio bora nchini.Imesema wafanyabiashara wengi wa nje, wamekuwa wakinunua bidhaa mashambani na kwa mfumo huo itasaidia kuzikuta bidhaa hizo katika eneo moja. Mkurugenzi Mkuu wa Tantrade, Edwin Rutageruka alisema hayo katika mkutano wa biashara ya matunda na mboga katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam(DITF) yanayoendelea katika Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Alisema Tantrade inawataka wakulima pamoja na wafanyabiashara nchini, kushirikiana nao ili kuweza kutatua changamoto ambazo wanakutana nazo katika shughuli zao.Alisema pamoja na mikakati ya mamlaka hiyo na wadau wengine ya kuendeleza bidhaa za Tanzania, yawapasa kutoa ushirikiano wa kutosha ili kutambulisha uwezo wa ubora wa kampuni katika kufanya biashara, waweze kutambulisha uwezo na ubora wa kampuni katika kufanya biashara ili waunganishe na fursa ambazo wanazipata.Aidha, Rutageruka alisema takwimu zinaonesha kuwa thamani ya mauzo ya bidhaa za viwandani, iliongezeka na kufikia dola za Marekani milioni 794.6 mwaka 2018 kutoka dola za Marekani milioni 693.7 mwaka 2017, sawa na ongezeko la asilimia 14.5. “Takwimu zinaonesha kuwa Tanzania ina takribani viwanda 49,243 ambavyo kati yake, 393 ni viwanda vikubwa vilivyopata usajili mwaka 2016/2017.Viwanda hivyo vilivyosajiliwa, miongoni wao vinavyozalisha bidhaa mbalimbali, ikiwemo usindikaji wa matunda na mboga lakini bado vinakabiliwa na ukosefu wa malighafi kutokana na upungufu wa uzalishaji wa ubora wa matunda, mboga, maua na viungo,” alisema. Rutageruka alisema Tanzania iko katika mwaka wa tatu wa utekelezaji wa mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano wa mwaka 2016/2017- 2020/2021, unaolenga kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya Watanzania. | 3 |
URA iliyoifungisha virago Yanga kwa mikwaju ya penalti, inacheza na Mtibwa Sugar iliyoifunga Simba bao 1-0 na kuwavua taji hilo, katika mchezo huo wa fainali ambao mgeni rasmi ni rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.Akizungumza mjini hapa nahodha wa URA, Simeon Massa alisema kuwa, kama hakutakuwa na mizengwe, basi taji hilo ni lao. Alisema kuwa wana matumaini ya kufanya vizuri katika mchezo wao huo wa fainali ikiwa hawatafanyiwa mizengwe.Aidha, alisema pambano lao la fainali dhidi ya Mtibwa siyo rahisi sana lakini wanajua kila mbinu za wapinzani wao.“Mtibwa tumeiyoana na tunaiheshimu wana wachezaji wadogo kama wa kwetu, lakini tumewasoma mbinu zao zote,” alidai nahodha huyo.“Kama waamuzi hawatopewa maagizo maalumu na kamati basi kombe litapokelewa pale Jinja na baadae kulitembeza jijini Kampala,” aliongeza.Endapo klabu hiyo ya URA itafanikiwa kulinyakua kombe hilo itakuwa klabu ya pili kutoka nchini humo kutwaa Kombe la Mapinduzi baada ya KCCA kulibeba mwaka 2014 baada ya kuifunga Simba bao 1-0 katika fainali.Mtibwa Sugar italazimika kucheza kufa au kupona ili kuhakikisha wanalibakisha kombe hilo kwenye ardhi ya Tanzania ikizingatia kuwa ndiyo timu pekee ya nyumbani iliyofanikiwa kuingia kwenye hatua hiyo.Simba ambao ni bingwa mtetezi wa kombe hilo tayari wameaga mashindano hayo baada ya kutolewa na Mtibwa Sugar kwenye nusu fainali kwa kichapo cha bao 1-0 lililofungwa na kinda la Kizanzibari Ibrahim Rajab Juma “Jeba”.Bingwa wa mashindano hayo atajinyakulia kombe kubwa sambamba na kifuta jasho cha Sh milioni 10 huku mshindi wa pili akijinyakulia Sh milioni 5.Mashindano hayo ni ya 10 tangu kuanza kutambulia rasmi mwaka 2007, Mtibwa ndiyo timu pekee iliyocheza fainali mara nne huku Simba ikiongoza kuchukua kombe mara tatu.Timu pekee ya Zanzibar iliyowahi kutwaa taji hilo ni Miembeni mwaka 2009 walipocheza fainali kule Gombani kisiwani Pemba dhidi ya mabaharia wa KMKM. | 4 |
TANZANIA imeweka rekodi ya dunia kwa ukusanyaji wa mapato, yatokanayo na sekta ya uchimbaji wa madini, hatua inayotokana na usimamizi mzuri wa rasilimali hiyo, ikichangiwa na mabadiliko ya sheria yaliyofanywa na serikali katika sekta hiyo hivi karibuni.Hayo yalielezwa jana na Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dk Hassan Abbas katika mkutano wake na waandishi wa habari Dar es Salaam jana.Alisisitiza kuwa hatua hiyo, imetokana na utendaji kazi wa ‘kisayansi’ wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli. Dk Abbas alisema katika kipindi cha miezi 11 kuanzia Julai, 2018 hadi juzi, serikali imeweza kuingiza Sh bilioni 302.63 za mapato hayo, ikiwa imesalia mwezi mmoja mwaka kukamilika.Alisema katika kipindi cha mwaka 2017 na 2018, kiasi cha Sh bilioni 301 za mapato hayo zilikusanywa ikiwa ni pungufu kwa wastani wa Sh bilioni moja zilizopatikana hadi sasa kwa mwaka huu unaoishia Juni.Aidha, alisema mwaka 2015/2016 kiasi cha Sh bilioni 210 zilipatikana kwa kipindi hicho ikilinganishwa na Sh bilioni 302 za msimu huu, suala alilosema kuwa kwa kiasi kikubwa limeonesha mafanikio katika sekta hiyo. Alisema kukusanywa kwa kiasi hicho cha fedha, kabla ya hata kukamilika kwa mwaka, kunatokana na usimamizi mzuri wa serikali katika sekta hiyo muhimu, ulioendana na kuanzishwa kwa masoko ya madini, miezi mitano tangu Rais Magufuli aagize uanzishwaji wake.Alisema hadi sasa kuna jumla ya masoko 24 ya madini, yaliyoanzishwa ndani ya kipindi cha miezi mitano, ambayo kimsingi yameonekana kufanya vyema katika ukusanyaji wa mapato hatua inayotoa matumaini. | 3 |
MSANII wa muziki nchini Richard Mavoko amekanusha taarifa kuwa aliwahi kwenda kupiga magoti ili kupata nafasi ya kurejea katika kundi WCB lililo chini ya msanii Nasib Abdul ‘Diamond Platnumz’. Mavoko aliachana na kundi hilo Julai mwaka jana kutokana na sababu ambazo hakuziweka wazi, licha ya Diamond kuwahi kusema kuwa msanii huyo alihitaji kuwa na kundi lake la Bilionare Kid hivyo alishindwa kumzuia. Kwa mujibu wa mahojiano yake na kituo cha redio cha Clouds Fm Mavoko alisema hajawahi na hatothubutu kuomba msamaha kwa lengo la kurejea katika kundi hilo na kuwataka mashabiki zake kupuuza taarifa hizo alizoziita za uzushi. “Mdogo wangu aliponitumia linki nikaona wao (Wasafi) ndo wanasema hivyo lakini mimi sijawahi kujaribu kufanya kitu kama hicho, niwaambie tu ndugu zangu wale waliokuwa wanategemea hicho hakiwezi kutokea, heri tu nibaki na nguo iliyochanika kuliko kuvua shati nibaki kifua wazi,”alisema Mavoko. Katika hatua nyingine msanii huyo alikanusha taarifa iliyotolewa na msanii Lulu Diva kuwa alimfanyia fujo nyumbani kwake baada ya kufanya kazi na kushindwa kumlipa. | 3 |
NA TWALAD SALUM, MISUNGWI MAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya ya Misungwi, mkoani Mwanza, imemhukumu msanii wa ngoma za asili, Mng’ahwa Kazanza (42), kwenda jela miaka 10 kwa kosa la kumiliki fisi wawili na kuwatumia kwenye sanaa zake bila kibali. Awali akisomewa mashtaka katika mahakama hiyo na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Doroth Mgenyi, ilielezwa mahakamani hapo kuwa mnamo Septemba 28, mwaka huu, kwenye Kijiji cha Sisu wilayani Misungwi, majira ya saa 7:30 mchana, Mng’ahwa Kazanza (42) alikamatwa akiwa na fisi wawili wenye thamani ya Sh milioni 4.8. Mara baada ya kusomewa mashtaka, msanii huyo alikiri kosa hilo na kudai alikuwa akiwatumia fisi hao katika sanaa zake bila kutambua kama ni kosa kuburudisha mashabiki wake kwa lengo la kuongeza kipato. Kutokana na kukiri huko, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ruth Mkisi, ilimtia hatiani kwa kosa la kupatikana na nyara za Serikali kinyume cha sheria Na. 5 ya mwaka 2009 na kumhukumu kwenda jela miaka 10 au kulipa faini ya Sh 4,840,000 ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaomiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Msanii huyo alishindwa kulipa faini hiyo na hivyo kwenda jela kutumikia adhabu hiyo ya miaka 10. | 1 |
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo jana Dar es Salaam, msimamizi mzalishaji wa Chaneli ya sinema zetu, Zamaradi Nzowa alisema Kiwanda cha Filamu ni mchakato wa kutafuta wasanii chipukizi kwa upande wa waigizaji na wapigapicha za video.“Mradi huu ulianza tangu mwanzoni mwa Machi mwaka huu tulipowakaribisha wadau kuwa wanaweza kutumia kazi zao kupitia mitandao yetu ya kijamii na hatimaye tulipata washiriki 200, walituma kazi zao,” alisema.Nzowa alisema lengo kuu la mradi huo ni kukuza na kuinua vipaji vya wasanii kutoka nchini ambao bado hawajapata fursa ya kuonesha kazi zao katika jamii. Alisema usaili huo utafanyika kuanzia leo kwenye fukwe za Coco, Dar es Salaam ambapo washiriki wataangaliwa vipaji vyao, na baadaye watachujwa na kubaki 20 ambao watashirikiana na wasanii wakongwe kwenye tamthilia hiyo itakayoanza kurushwa kuanzia Juni.Aliwataja majaji katika usaili huo kuwa ni msanii Susan Humba ‘Natasha’ , na Mhadhiri msaidizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Issa Mbura, ambao watafanya kazi ya kuchagua waigizaji bora chipukizi kisha baadaye kuwapa mafunzo kabla ya kuanza kuigiza. Naye Mkuu wa Masoko na Mauzo wa Azam Media, Mgope Kiwanga aliwataka wale watakaopata nafasi hiyo kuchangamkia fursa na kuhimiza wale ambao hawatabahatika wasikate tamaa. “Hii ni fursa pekee kwa vijana wa Kitanzania kutumia nafasi hii kuonesha vipaji vyao,” alisema. | 4 |
Dk Mukangara alisema hayo jana katika hotuba yake iliyosomwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Elisante ole Gabriel wakati wa uzinduzi wa michuano ya Airtel Rising Star kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.Alisema ni jukumu la kila mtu kuendeleza michezo kwa nafasi yake na kuongeza kuwa serikali imeweka mifumo ambayo itasaidia kila mdau wa michezo anayetaka kuendeleza sekta hiyo anafanya hivyo.Alisema kampuni zikifanya hivyo zitatangaza bidhaa zao kwa bei rahisi kwa kuwa watatangazwa na vyombo mbalimbali vya habari. Akizungumzia kuhusu michuano hiyo, alisema inawajengea uwezo zaidi vijana katika kujiendeleza kimichezo na kuwa na faida kubwa kwa sekta hiyo baadaye.Alisema michuano ya Airtel Rising Stars imesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza soka la wanawake na hivyo kufanya vyema kwenye michuano mbalimbali ya kimataifa. Alisema serikali kwa upande wake inatimiza majukumu ya kuendeleza soka kwa ujumla wake na kuitaka sekta binafsi nayo kuendeleza michezo.“Mimi ninachoweza kuwaomba kwa sasa wadau wengine wajitokeze kuanzisha na kuendeleza michuano kama hii yenye kuinua vipaji vya vijana na hiyo inawezekana kama makampuni hayo yakiamua,” alisema Dk Mukangara.Aliongeza kuwa “changamoto zinazokwaza kupatikana kwa mafanikio ya michezo zinatakiwa kutatuliwa haraka na wizara inaweza kuwasaidia kwa hali na mali katika kutatua changamoto hizo.” Michuano hiyo inayoshirikisha timu za wanawake na wanaume ambapo zimegawanywa katika makundi manne.Katika kundi A la wanaume kuna timu kutoka Morogoro, Kinondoni na Mwanza huku kwa upande wa timu za wanawake za kundi hilo kuna timu za Temeke, Arusha na Mwanza. Kundi B wanaume ni Ilala, Mbeya na Temeke huku kwa timu za wanawake zilizopo ni Mbeya Ilala na Kinondoni. | 4 |
WATU watatu akiwemo mwanamke mmoja wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kutokana na tuhuma za kupatikana na vipande 20 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh milioni 87.Kwa mujibu wa jeshi hilo kupitia kwa Kamanda wa Kanda hiyo Lazaro Mambosasa, kukamatwa kwa watu hao wanaotajwa kujishughulisha na biashara hiyo ya nyara za serikali, kumetokana na taarifa iliyolifikia jeshi hilo kutoka kwa wasamaria. Wanaoshikiliwa kutokana na tukio hilo ni pamoja na Salehe Idd (57), mkazi wa Vingunguti, Waziri Ibrahimu (40), mkazi wa Vingunguti na Bertha Nelson (38) mkazi wa Yombo.“Watuhumiwa hao wanaendelea kuhojiwa kwa kushirikiana na maofisa wa Maliasili na Utalii na upelelezi ukikamilika watapelekwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili,” alisema Kamanda Mambosasa. Katika tukio jingine, jeshi hilo limekamata silaha mbili aina ya shotgun pump action zenye namba za usajili P-913581 TZ CAR 76456 na P-625302 TZ CAR 76467 pamoja na risasi 17 zikiwa zimetelekezwa katika eneo la Kinyerezi Kanga.Aidha, Kamanda Mambosasa pia aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za wahalifu kupitia kwa namba yake ambayo ni 0715009983, Kamanda wa Ilala ACP Salum Hamduni kwa namba yake ambayo ni 0715009980, Kamanda wa Temeke ACP Jumanne Muliro kwa namba 0719009976 na Kamanda wa Kinondoni ACP Emmanuel Lukula kwa namba 07150099979. | 3 |
Mohamed Hamad Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti ameagiza Jeshi la Polisi wilayani Kiteto kuwakamata wanachimbaji wa madini aina ya rubi, Kijiji cha Orgine kwa kufanya shughuli hiyo kinyume cha sheria. Mnyeti ametoa agizo hilo baada ya lalamikiwa na wananchi
hao kuwa hawanufaiki na shughuli ya uchimbaji wa madini Kijijini hapo huku
wachimbaji wakiendelea kuneemeka. Akiwasilisha kero hiyo, Jafari Yasini amesema, kijiji cha
Orkine hakinufaiki na uchimbaji, hata vifusi vya kufukia msingi katika miradi
ya ujenzi wanalazimika kununua kutoka kwa wachimbaji hao. Mkuu wilaya ya Kiteto Tumaini Magessa, alipoulizwa kuhusu
suala hilo alisema kuwa, wilaya ilishawaandikia barua wachimbaji na kushangazwa
kusikia lalamiko hilo kuwa kazi hiyo inaendelea. “Tuliwaandikia barua hawa wachimbaji wa madini aina ya rubi
hapa Kijiji cha Orkine baada ya kubaini kuanza kunufaika na madini haya ingawa
hawataki kuonyesha nufaiko hilo wakidai bado wako kwenye majaribio kipindi
chote”alisema Magessa. Akitoa agizo hilo Mnyeti alimwagiza Mkuu wa Polisi Kiteto,
Fadhili Luoga kuwakamata wachimbaji hao mara moja na kuandaliwa mashitaka ili
waweze kujibu tuhuma kwanini waendeleze uchimbaji kinyume cha sheria. “OCD ninakuagiza nenda ukawakamate hawa wachimbaji wa
madini haya, haiwezekani waendelee kuchimba kwa zaidi ya miaka 20 bila kulipa
kodi hali hii halikubaliki hata kidogo”me sema Mnyeti. | 3 |
NA RHOBI CHACHA AKIWA na wapambe 15 msanii wa Bongo Fleva, Nurdin Bilali ‘Shetta’, alilazimika kutumia nguvu za ziada ili kuingia na wapambe wake hao katika shoo ya kuadhimisha miaka 16 ya muziki kwa msanii Juma Nature, iliyofanyika katika Ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala jijini Dar es Salaam. Shetta ilimlazimu kufanya uamuzi huo baada ya njia yake ya kutishia kususia kufanya onyesho lake katika onyesho hilo kupuuzwa huku akikataliwa kuingia na idadi hiyo kubwa ya wapambe wake badala yake alitakiwa aingie na wapambe nane tu. Kabla ya Shetta kutumia nguvu, wapambe wake nane waliokubaliwa kuingia ukumbini walimtaka msanii wao huyo waondoke kama wenzao hawatakubaliwa kuingia huku wakilalamika kwamba mbona msani Nassib Abdul ‘Diamond’ huwa na wapambe wengi lakini hawawazuii. “Hapa kwa vile Shetta mnamzuia lakini angekuwa Diamond angeingia na wapambe wake hata ishirini na msingemzuia kwanini Shetta bora tusepe,” alipaza sauti mmoja wa wapambe hao. Hata hivyo, Shetta alipohojiwa alishangazwa na kukataliwa wakati huwa anaongozana na wapambe 15 katika kila onyesho lake, lakini hata hivyo onyesho lilifanyika kwa mafanikio na Nature akafurahia miaka yake 16 huku kituo cha EFM kikisherehekea mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake. | 1 |
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen amesema Sh bilioni 5.5 zimepokelewa kutoka serikali kuu kwa ajili ya ukarabati na ujenzi mpya wa miundombinu ya kutolea huduma za dharura kwa wajawazito na watoto wachanga (CeMONC) katika vituo vya afya 13. Dk Kebwe alisema hayo mjini Ifakara jana katika taarifa yake kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati wa ziara yake mkoani Morogoro. Mkuu wa mkoa alivitaja vituo vya afya vilivyopokea fedha hizo na halmashauri za wilaya zake katika mabano kuwa ni Mtimbira na Ngoheranga ( Malinyi), Kibati ( Mvomero), Mkuyuni , Mikese, Kinonko , Duthumi na Kisemu (Morogoro). Vituo vingine vilivy- opata fedha hizo ni Gairo (Gairo),Mlimba na Mchombe ( Kilombero), Lupiro ( Ulanga), Kidodi, Mikumi na Malolo ( Kilosa) .“Vituo hivi vyote ukiacha cha Malolo wilayani Kilosa, vimepokea fedha kutoka serikali kuu jumla ya Sh bilioni 5.5,” alisema Dk Kebwe.Alisema hadi sasa vituo vya afya vya Kibati, Mtimbira, Kidodi , Mikumi , Gairo, Mlimba na Mang’ula wananchi wameshaanza kupata huduma kwenye majengo mapya . Dk Kebwe alisema vituo vyote vitakapokamilika, mkoa utakuwa na vituo vya afya 25 venye uwezo wa kutoa huduma za dharura sawa na asilimia 48 ya vituo vyote vya afya vilivyopo mkoani humo. “Lengo ni kufikia asilimia 70 ya vituo vyote vya afya vitakavyokuwepo vyenye uwezo wa kutoa huduma za upasuaji ifikapo Desemba mwakani, ”alisema. Dk Kebwe alisema Sh bilioni 1.5 zimetolewa kwa kila mmoja, Wilaya ya Mvomero imepatiwa Sh milioni 500 na hivyo kufanya fedha iliyopokelewa kufikia Sh bilioni tano. Akizungumzia usimamizi wa huduma za dawa, alisema mkoa unaendelea kufanya usimamizi na hali ya upati- kanaji wa dawa imeendelea kuimarika hadi kufikia asilimia 92.7 Juni, mwaka huu. “Tunatoa shukrani za dhati kwa serikali kwa kutoa Sh bilioni 3.3 kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa mwaka 2018/19,” alisema Dk Kebwe. | 3 |
Kwa pointi hizo, Yanga imeiivua ubingwa Azam FC, kwani timu hiyo ya Chamazi inao uwezo wa kufikisha pointi 54 tu katika mechi zake tatu zilizobaki kukamilisha msimu huu.Yanga imetangaza ubingwa jana baada ya kuibugiza Polisi Morogoro kwa mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku mshambuliaji wa zamani wa Simba, Amissi Tambwe akifunga mabao matatu ‘hat-trick.’Mabingwa hao wa kihistoria wa Bara ambao wamefikisha rekodi ya kutwaa taji mara 25 kama Bayern Munich ya Ujerumani juzi, ilitwaa taji hilo kwa mara ya mwisho mwaka 2013. Simba inayoifuatia imetwaa taji hilo mara 18.Kwa ubingwa huo, Yanga sasa watarejea katika nafasi ya kuiwakilisha nchi katika Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya msimu huu kushiriki Kombe la Shirikisho kutokana na kumaliza nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya Azam FC. Yanga imetawazwa bingwabaada ya kufikisha pointi 55, ikishinda mechi 17, ikitoka sare mara nne, kufungwa mara tatu na kufunga mabao 51 huku ikifungwa 15.Imebakiza mechi mbili dhidi ya Azam FC utakaochezwa Mei 6 na kumaliza ligi kwa kuikabili Ndanda FC mjini Mtwara, Mei 9. Tangu ilipofungwa na Simba, Machi 8, mwaka huu kwa bao 1-0, Yanga haijapoteza mechi yoyote ikicheza mechi nane mfululizo ikiondoka na ushindi.Tambwe alifunga bao safi la kwanza katika dakika ya 41 akiunganisha krosi safi ya Simon Msuva na kuasha nderemo kwa mashabiki wa Yanga upande wa kusini unaokaliwa na mashabiki wa klabu hiyo ya Jangwani.Polisi walianza kipindi cha pili kwa nguvu na dakika nne walimtoa mshambuliaji wa Yanga anayecheza kwa mkopo, Said Bahanuzi na kumuingiza Nicholaus Kabipe, lakini mabadiliko hayo hayakuisaidia na badala yake Yanga walipata bao katika dakika ya 53 likifungwa tena na Tambwe akimalizia mpira uliotemwa na kipa wa Polisi, Abdul Ibad.Mpira wa bao hilo ulianzia kwa Msuva aliyepiga shuti kali lililotemwa na kipa huyo na mpira kumkuta mfungaji aliyeujaza wavuni na hapo, sherehe za ubingwa kwa mashabiki wa Yanga waliofurika uwanjani zikaanza.Tambwe alijihakikishia kuondoka na mpira baada ya kufunga bao la tatu kwa kichwa akikamilisha ‘hat-trick’ katika dakika ya 59 akiunganisha krosi ya Mrisho Ngassa.Ubingwa ulikamilishwa sare Yanga katika dakika ya 66 baada ya Msuva kufunga bao la nne kwa shuti kali baada ya akiwahi pasi murua ya kupenyezewa na Ngassa ambaye hakuwa mchoyo katika kutengeneza nafasi za kufunga jana. Kwa bao hilo, Msuva amezidi kujiweka pazuri kutwaa Kiatu cha Dhahabu akiongoza kwa kufunga mabao 17 wakati Tambwe anamfuatia akiwa na mabao 14. Moja alilifunga akiwa Simba.Bantu Admin aliifungia Polisi Moro bao la kufutia machozi katika dakika ya 83 baada ya kupiga shuti kali lililogonga ‘mtambaa panya’ kabla ya kutinga wavuni baada ya kumshinda kipa Deogratius Munishi ‘Dida.’Wakati Yanga ikiwa imeshajihakikishia ushindi huo, Mkuu wa Idara ya Habari wa Yanga, Jerry Muro alianzisha sherehe za ubingwa kwa kufungua mvinyo, huku mashabiki wakiwa na fulana zilizoandikwa ‘Yanga bingwa 2014/15…ubingwa wa mapema zaidi.’Mara baada ya pambano kumalizika, wachezaji wa Yanga wakiongozwa na kocha wao mkuu, Hans van der Pluijm walizunguka uwanja kuwapongeza mashabiki wao wakiwa na fulana zilizoandikwa ‘Yanga Bingwa 2014-2015.’Vita sasa imebaki katika kusaka nafasi ya pili, ambapo Azam FC na Simba ambazo zitacheza mwishoni mwa wiki, kila moja inawania nafasi hiyo, huku Azam ikiwa na pointi 45 wakati Wekundu wa Msimbazi wana pointi 41.Mbali na nafasi hiyo, pia vita kali nyingine iko katika kupigania kutoshuka daraja, ambapo Ndanda FC, Polisi Moro, Tanzania Prisons kila moja ina pointi 25 pamoja na timu nne zenye pointi 28, zikipigana vikumbo kuepuka kushuka.Yanga: Munishi, Juma Abdul, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Kelvin Yondani, Said Juma, Msuva/ Jeryson Tegete, Haruna Niyonzima/ Nizar Khalfan, Tambwe/ Hussein Javu, Ngassa na Kpah Sherman. Polisi Moro: Ibad, Ally Teru, Hassan Mganga, Meshack Abel/ Bakari Nahodha, Laban Kambole, Anafi Selemani, Bantu, Said Mkangu, Bahanuzi/Kabipe, Seleman Kassim na James Abrose/Mussa Mohamed. | 4 |
KOCHA wa Simba, Patrick Aussems amesema bado yupo kwa wekundu hao na leo anatarajiwa kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya kujiandaa na mchezo ujao dhidi ya Ruvu shooting.Aussems aliomba ruhusa kwa mabosi wake Simba kuwa anatoka kidogo na atarejea baada ya siku mbili kitendo kilichotafsiriwa tofauti na baadhi ya watu wakidai huenda ameachia ngazi.Taarifa aliyotoa jana, kocha huyo raia wa Ubelgiji alisema: “Nimetoka kidogo kwa sababu zangu binafsi, nitarudi kesho (leo) kujiandaa na mchezo ujao dhidi ya Ruvu”.Alisema mchezo ujao una umuhimu mkubwa kwao kuhakikisha wanapambana na kupata pointi tatu. Hata hivyo, Mtendaji Mkuu wa Simba, Senzo Mazingisa alikiri kocha huyo alitoa taarifa kupitia barua pepe kuwa anatoka kidogo kwa sababu ana dharura ila hakusema anakwenda wapi.“Aussems alinitumia barua pepe Jumatatu asubuhi na kusema kuwa amepata dharura anaondoka ila hakusema anakwenda wapi,”alisema.Mtendaji huyo alisema labda atakaporejea atakuwa na maelezo ya kutosha juu ya safari ya kocha huyo huku akisisitiza kuwa bado kocha huyo ni mwajiriwa wa klabu hiyo.Kutokuwepo kwa kocha huyo hakuzuii programu zao kwani jana usiku walikuwa na mechi ya kirafiki dhidi ya JKT Tanzania ikiwa ni sehemu ya maandalizi yao kuelekea mchezo ujao wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara.Tayari wekundu hao ukiachilia mchezo huo, walicheza pia na KMC kujipima nguvu na kula kichapo cha mabao 2-1. | 4 |
TIMU tatu za vikosi vya SMZ juzi vilitoka kidedea katika michezo yao ya Ligi Kuu ya Zanzibar iliyopigwa kwenye viwanja tofauti.Timu hizo ni KVZ ambayo iliifunga Mwenge mabao 2-1, JKU iliyoisambaratisha Jamhuri kwa bao 1-0 na Mafunzo iliyoipeleka puta Mbuyuni kwa kuikandika mabao 3-0.KVZ na JKU zilishuka katika Uwanja wa Amaan saa 8:00 mcahna na saa 10:00 Mafunzo ilishuka katika dimba la Mao Dze Tung saa 10:00 Jioni.Katika mchezo uliowakutanisha KVZ na Mwenge, mabao yake yalifungwa na Ayoub Lipati dakika ya nane na Abdul Yussuf dakika ya 26 wakati bao la kufutia machozi la Mwenge liliwekwa kimiani na na Jumanne Alawi katika dakika ya 52. Kwa upande wa timu ya JKU iliyoshuka uwanjani hapo saa 10:00 za jioni, bao lake la pekee liliwekwa kimiyani na Mbarouk Chande katika dakika ya 46.Licha ya kushinda kwa vikosi hivyo pia vimerudi tena katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya kwanza ili kuwa mabingwa baada ya kuingia katika hatua ya tatu bora kwenye msimamo wa ligi hiyo.Aidha, huko kisiwani Pemba katika Uwanja wa Gombani saa 8:00 mchana, Selem ilionja machungu kwa kufungwa mabao 2-0 na Mlandege, huku wa saa 10:00 jioni Polisi ikafungwa na Chipukizi kwa idadi kama hiyo ya magoli.Chipukizi kwa ushindi huo imefikisha pointi 23 na kuwa katika nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi hiyo wakati Polisi bado wapo katika nafasi ya 10 wakiwa na pointi 35.Kwa mujibu wa msimamo wa ligi hiyo, KMKM inaongoza ikiwa na pointi 55 wakifuatiwa na KVZ ambao nao wana pointi 55, JKU inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 54 wakati Malindi inashika nafasi ya nne ikiwa na pointi 53.Nafasi ya tano kwa sasa inashikiliwa na Mafunzo wenye pointi 50 wakati Mlandege wapo nafasi ya sita wakiwa na pointi 48, huku Zimamoto wanashika nafasi ya saba wakiwa na pointi zao 45 na Chuoni ipo nafasi ya nane pointi 38.Kwa mujibu wa msimamo huo bado timu sita za Pemba zipo katika mstari mwekundu ikiwemo Mwenge yenye pointi 20 nafasi ya 14, New Star 20 nafasi ya 15, Mbuyuni nafasi ya 16 pointi 16, Hard Rock wa 17 pointi 14, Opec wa 18 pointi 14 na Kizimbani inashika mkia nafasi ya 19. | 4 |
Na MWANDISHI WETU, WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amezindua mradi wa maji safi na salama katika Kijiji cha Jobaj, Wilaya ya Karatu mkoani Manyara, unaotekelezwa na Shirika la World Vision Tanzania. Mradi huo wenye thamani ya Sh milioni 285, ulizinduliwa juzi wakati wa ziara ya kiongozi huyo mkoani hapa na utahudumia vijiji vitatu vya Kata ya Baray ambavyo ni Mbunga Nyekundu, Jobaj na Dumbechand. Akizungumza baada ya uzinduzi huo, Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka wananchi wautunze ili uweze kudumu kwa muda mrefu. “Nawaomba muutunze mradi huu kwa sababu kama utadumu kwa muda mrefu, ile kero ya maji iliyokuwa ikiwakabili itakuwa imeondolewa,” alisema. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miradi wa World Vision Tanzania, Revocutus Kamara, alisema mradi huo unatokana na mahitaji ya maji katika vijiji hivyo vitatu na uwepo wa kisima kirefu cha maji kilichochimbwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia mwaka 2009. “Mradi huu wa maji unatekelezwa kwa awamu tatu. Awamu ya kwanza ilianza Machi hadi Novemba 2016, ambapo wakazi 5,272 ikiwa ni pamoja na taasisi nne za Serikali ambazo ni zahanati, magereza, shule ya msingi na sekondari zilizoko katika Kijiji cha Jobaj, wananufaika kwa kupata maji safi na salama. “Awamu ya pili na ya tatu ya mradi huo itaanza Desemba hii, na itagharimu zaidi ya Sh milioni 200,” alisema Kamara. Akizungumza kuhusu mradi wa umwagiliaji, mkurugenzi huyo alisema shirika lao limechangia kuboresha miundombinu ya umwagiliaji kwa kujenga kilomita 1.716 za mfereji katika Kijiji cha Jobaj. | 3 |
['Aston Villa kumsajili mshambuliaji wa Genk na Tanzania kwa dau la £10m', 'Aston Villa inatumai kukamilisha makubaliano ya dau la £10m kumsajili mshambuliaji wa Genk Mbwana Samatta huku mkufunzi Dean Smith akilenga kuimarisha safu yake ya mashambulizi.', 'Dean anahitaji kuimarisha safu hiyo baada ya kumpoteza mshambuliaji wa Brazil Wesley kwa kipindi chote cha msimu kilichosalia na jeraha la goti alilopata katika mechi dhidi ya Burnley wakati wa siku ya mkesha wa mwaka mpya.', 'Samatta, ambaye alifunga dhidi ya Liverpool katika mechi ya klabu bingwa Ulaya msimu huu ameonekana kulengwa na Villa.', 'Hatahivyo maelezo ya ndani kuhusu uhamisho huo bado hayajaafikiwa. ', 'Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kutoka Tanzania anahitaji kibali cha kufanya kazi hivyobasi hatapatikana katika mechi ya ugenini ya Villa dhidi ya Brighton siku ya Jumamosi. ', 'Villa iko tayari kumuuza mshambuliaji wa Ivory Coast Jonathan Kodija na tayari timu ya ligi ya mabingwa nchini England Nottingham Forest na ile ya Ligui 1 ya Ufaransa Amiens zikimnyatia .', 'Klabu hiyo ya Dean Smith ipo katika nafasi ya 18 katika ligi ya Premia baada ya kucheza mechi 22.', 'Villa pia imehusishwa na usajili wa mshambuliaji wa Leicester Islam Slimani mwenye umri wa miaka 31. ', 'Mchezaji huyo wa Algeria kwa sasa yuko kwa mkopo akiichezea Monaco , na Smith alisema kwamba klabu hyo italazimika kujaribu kupata usajili. ', "''Mwezi wa Januari ni mgumu sana bila kuwepo na washambuliaji wazuri kwa kuwa klabu zinaweza kupandisha bei , limekuwa dirisha gumu la uhamisho na tutalazimika kufanya kitendo cha kijasiri'., alisema Smith. ", "''Mimi nimetulia na nina matumaini tutapata wachezaji lakini tuna mechi kubwa , na iwapo hatutapata mshambuliaji mmoja kufikia Jumamosi itakuwa mara ya tatu mfululizo bila mshambuliaji anayetambulika''..", "''Lazima tuhakikishe kwamba tunafanya vyema na tunatumai tutapata mshambuliaji mmoja. Kuna haraka ya kupata mchezaji huyo''. ", "''Huku Wesley akipata jeraha na Keinan Davis akiwa nje lazima tujiimarishe vilivyo hivyobasi tunatafuta wachezaji kadhaa''. "] | 4 |
KATIBU Mkuu Kiongozi, ambaye pia ni Mkuu wa Utumishi wa Umma, Balozi John Kijazi amewaagiza Makatibu Wakuu kuhimiza michezo mahala pa kazi kwa vitendo ili kuwa na watumishi wa Umma wenye afya njema.Kauli hiyo iliwakilishwa jana na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Maimuna Tarishi aliyemwakilisha Balozi Kijazi katika Bonanza la Michezo lililoandaliwa na Shirikisho la Michezo ya Wizara, Idara, Wakala wa Serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa (Shimiwi), na kufanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri hapa.Kijazi alisisitiza kuwa michezo ni kazi na kazi ni michezo, ambapo sasa Makatibu Wakuu waweke mazingira yatakayowezesha watumishi wa umma kupitia taasisi zao, waweze kushiriki kwenye michezo mbalimbali, ambayo inajenga umoja na ushirikiano baina ya watumishi.“Haya ni maagizo ya Katibu Mkuu Kiongozi amenituma nije niseme kwa kuwa yupo katika kazi nyingine, wito ni kwa Makatibu Wakuu wote na wakuu wa taasisi kuhakikisha wanaweka mazingira wezeshi yatakayowezesha watumishi kufanya mazoezi mara kwa mara na hata katika michezo kama hii ya Shimiwi,” alisema Tarishi akimnukuu Kijazi.Alisema sasa muwekwe utaratibu kwa Watumishi wa Umma kushiriki michezo ambayo haitatumia gharama kama wanavyodhania wengine.“Kwa waajiri hatuna budi kuweka mazingira rafiki ya kuwawezesha Watumishi kuwa na utaratibu wa kushiriki kwenye michezo yeyote na hii inafanyika bila gharama yeyote kabisa, kwani wakati mwingine tunakimbilia hatuna fedha au hatujatenga fungu katika bajeti wakati hata hapa ukiangalia hakuna gharama kubwa iliyotumika,” amesisitiza Kijazi.Amewataka watumishi wa umma kufanya mazoezi kila wakati ili kujiweka katika afya kwa wakati wote, ambayo itawasaidia kufanya kazi kwa weledi.Ametoa maagizo kwa viongozi wa Shimiwi, kwa kuwa sasa wameanza kufufua michezo hiyo baada ya kusimama kwa muda mrefu, na sasa waendelee mbele kwani yanawakutanisha watumishi wa maeneo mbalimbali ya kazi ya serikali na husaidia kubadilishana uzoefu.Hatahivyo, amesema michezo ni nidhamu hivyo kuwe na nidhamu kwenye michezo kwani kutasaidia watumishi kufanya kazi kwa bidii na kuwa na ubinifu wa hali ya juu. Mwenyekiti wa Shimiwi, Daniel Mwalusamba alisema wachezaji wanahimizwa kufanya mazoezi kwa ajili ya kujenga, kulinda na kuimarisha afya zao.“Michezo ni kazi, hivyo wanapaswa kuzingatia taratibu na miongozo inayokuwa imetolewa kila wakati na serikali, na kama agenda ya kitaifa ilivyo ya kujenga Tanzania ya Viwanda, na ili tufanikiwe tunahitaji kuwa na Watumishi wenye afya bora wanaoweza kufanya majukumu yao kwa wakati na kushiriki michezo, ambapo sasa wanaweza kuandaa mabonanza sehemu za kazi kwa siku za mwishoni mwa wiki,” amesema Mwalusamba.Katika michezo iliyochezwa jana kwa upande wa kuvuta kamba wanaume, timu ya Waziri Mkuu walitolewa jasho na Mambo ya Ndani baada ya kulazimishwa sare ya mvuto 1-1 wakati katika netiboli, timu ya Utumishi imechapwa na Tamisemi magoli 24-17 huku Afya wakiwashinda GST kwa magoli.Katika mchezo wa soka, Utumishi wamewachapa Afya magoli 2-0, huku Ardhi wakiwapeleka puta ofisi ya Mwanasheria Mkuu kwa magoli 4-0. | 4 |
Mwandishi wetu –Tanga MENEJIMENTI ya uongozi wa hoteli yenye
hadhi ya nyota tano ya Tanga Beach Resort iliyoko jijini Tanga, imelazimika
kufunga hoteli hiyo ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kuzuia mikusanyiko
ili kujikinga na ugonjwa wa corona unaotokisa dunia kwa sasa. Akizungumza na waandishi wa habari juzi
jijini hapa, Meneja wa hoteli hiyo, Joseph Ngonyo, alisema kuwa wameamua kuifunga
kutokana na mlipuko wa ugonjwa huo hapa nchini pamoja na kudhibiti mikusanyiko
ya watu Alisema kuwa awali tayari biashara ya
hoteli ilianza kusuasua kutokana na uwepo wa ugonjwa huo, hivyo kulazimika
kufunga ili kuzuia mkusanyiko wa watu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea
katika msimu wa sikukuu. “Dunia sasa hivi na hata nchini kwetu
kumekuwa na tatizo la gonjwa la corona, hivyo tumeamua kusitisha huduma ili kuunga
mkono kauli ya Serikali ya kuzuia mkusanyiko wa watu wengi pamoja, hivyo ili
kuwadhibiti tumelazimika kufunga hoteli hiyo,” alisema Ngonyo. Aidha aliwataka wananchi kuacha dhana
potofu ambazo zimeanza kusambaa katika mitandao ya kijamii na kwamba wameamua
kuunga mkono juhudi za Serikali hivyo shughuli za hoteli zinatarajiwa kuanza
tena mwishoni mwa Mei. Mmoja wa wafanyakazi katika hoteli hiyo,
Hadija Ramadhani, alisema kuwa wamelazimika kuunga mkono maagizo ya Serikali
ili kupunguza maambukizi kwa wafanyakazi pamoja na wananchi ambao wanaweza
kufika katika hoteli hiyo kupata huduma. “Tunaomba watu waachane na habari za
mitandao kwani zinatuchafua, lakini lengo letu ni kuhakikisha usalama wa
wafanyakazi wetu pamoja na wateja ambao wanakuja kupata huduma katika hoteli
yetu,” alisema Hadija. | 3 |
RAMADHAN HASSAN -DODOMA WAZIRI wa
Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, George Mkuchika, amezitaka
wizara pamoja na taasisi zote kuhakikisha zinawalipa mishahara pamoja na
stahili zote watumishi ambao wamepandishwa madaraja kulingana na nafasi walizo
nazo sasa. Pia ameagiza
upandishaji wa madaraja kwa watumishi na wapewe nafasi ya upendeleo wale ambao
wanakaribia kustaafu. Hatua hiyo
imekuja kutokana na wajumbe wa Baraza Kuu la Nne la Wafanyakazi katika Utumishi
wa Umma kumlalamikia kwamba baadhi ya watumishi wamekuwa wakipandishwa
madaraja, lakini hawalipwi stahiki zao. Akizungumza
na waandishi wa habari Dodoma jana wakati akizindua na kufungua mkutano wa
baraza hilo, Waziri Mkuchika
alisema kumekuwa na malalamiko
katika maeneo mbalimbali nchini kuwa watumishi ambao Serikali ilitoa maagizo
kuwa wapandishwe madaraja, mishahara yao imebaki kama ilivyokuwa awali. “Nilikuwa
mkoani Ruvuma, huko pia nimekutana na malalamiko ya kutosha, kila mtumishi
analalamika kuwa kapanda daraja, lakini mshahara bado haujapanda,” alisema
Mkuchika. Alisema
kutokana na hali hiyo, viongozi wa Serikali wanaohusika na suala hilo
wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanalifanyia kazi ili kuweza kuwapatia stahili zao
watumishi wote waliopanda madaraja. Pia aliagiza
katika upandishaji wa madaraja kwa watumishi, wapewe nafasi ya upendeleo wale
ambao wanakaribia kustaafu. “Serikali
ilitangaza upandishaji wa madaraja kwa wale wenye sifa, lakini pia wanaotakiwa
kupatiwa kipaumbele ni wale ambao wanakaribia kustaafu katika utumishi wa umma
ili waweze kupata stahiki ambazo zitawawezesha kujikimu kule wanakokwenda,”
alisema Mkuchika. Alisema Novemba mosi, 2017, Serikali iliidhinisha
watumishi wapatao 85,000 waliokasimiwa katika bajeti ya mwaka 2015/16
kupandishwa vyeo. “Awamu
nyingine ya upandishaji wa vyeo imefanyika Mei 1, 2019 ambapo watumishi 193,166
waliokasimiwa katika bajeti ya mwaka 2017/18 wamepandishwa vyeo,” alifafanua
Mkuchika. Aliwapongeza
watumishi wote wa umma nchini ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kukusanya
na kusimamia mapato ya Serikali ambayo yanatumika katika kuboresha miundombinu
mbalimbali. “Nyie ndiyo
mmekuwa mkikusanya haya mapato ya Serikali, niwapongeze kwa kiasi kikubwa kwani
hapo zamani kabla ya hii awamu ya tano, tulikuwa tukikusanya kwa mwezi kiasi
cha Sh bilioni 800, lakini hivi sasa
imefikia hadi Sh trilioni 1.7 kwa mwezi kiasi ambacho tunatakiwa kushikilia
hapohapo,” alisema. Aliwataka
watumishi wa umma waliopo chini ya Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora,
kuhakikisha wanakuwa wa mfano katika suala la kupinga rushwa na kufanya kazi
kwa uadilifu bila ya kuchagua maeneo ya kwenda kufanya kazi. “Rushwa
katika ofisi za umma imekuwa kikwazo kwa wananchi wetu tunaowatumikia, naomba
katika ofisi yangu watumishi wangu muwe watu wa mfano, ambao mtakuwa
hamjihusishi na rushwa hata kidogo ili kuakisi jina la utawala bora,” alisema. Makamu
Mwenyekiti wa Baraza hilo, Leah Ulaya, alisema changamoto ambazo zimekuwa kero
kwa watumishi ni upandishwaji wa madaraja bila kuzingatia stahiki nyingine
ikiwemo mishahara. “Tunakuomba
mheshimiwa waziri suala hili lifanyiwe kazi ili sisi watumishi ambao tumepata
fursa ya kupanda madaraja tuweze kupata stahiki zetu kulingana na miongozo ya
utumishi wa umma,” alisema Ulaya. | 3 |
WANAFUNZI sita, kati ya 25, waliopigwa na radi katika Shule ya Msingi Emaco Vision English Medium mkoani Geita, wamekufa katika hospitali ya mkoa walikolazwa kwa ajili ya matibabu.Wakati tukio hilo likitokea, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), wametoa mwito kwa jamii na wajenzi wa majengo nchini, kuhakikisha wanaweka vizuia radi kwa majengo yote hata kama hayana umeme ili kuepusha madhara ya radi kwa binadamu na mali.Ajali hiyo ya kusikitisha ilitokea jana saa tatu asubuhi katika Kata ya Nyankumbu mjini Geita wakati mvua zikiendelea kunyesha, zilizoambatana na ngurumo za radi zilipiga na kusababisha maafa hayo.Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Geita, Josephat Maganga alisema taarifa za awali alizopata saa nne asubuhi hapo jana, ni kwamba radi hiyo iliwajeruhi watoto 25 ambao walikimbizwa hospitali ya mkoa kwa ajili ya matibabu.Hata hivyo, alisema baadaye walipewa taarifa na uongozi wa hospitali hiyo kuwa watoto sita kati ya 25 waliojeruhiwa na radi hiyo wamefariki kutokana na majeraha ya radi hiyo.“Nilipata taarifa kuhusu tukio hilo ingawa niko likizo kidogo ila nilifuatilia na kupewa taarifa hiyo, tumepoteza watoto wetu wadogo sita hadi sasa, na taarifa zaidi tutaendelea kuzitoa kadri hali itakavyokuwa, ila ni kweli radi ilipiga na kuleta maafa hayo,” alisema Maganga.Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo alisema majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo. Akifafanua zaidi, Maganga alisema tukio hilo liliwakumba wanafunzi wa darasa la pili na tatu na pia walimu wawili walijeruhiwa.Aliwataja waliokufa ni Jacqueline Josephat, Christina Erick, William Emil, Lulu Gilbert, Abdul Bundala na Yusra Hauni, na kwamba wanafunzi wengine 21 na walimu wawili wamejeruhiwa.Ofisa Elimu ya Msingi mkoani humo, Yese Kanyuma alisema radi hiyo ilitokea wakati wanafunzi hao wakiwa darasani hadi sasa majeruhi walio hospitalini ni 25. Akizungumzia radi na jinsi ya kujikinga nayo, Fundi Sanifu Jiolojia wa GST, Christina Andrea alisema Tanzania imepakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ambayo ni kitovu cha radi kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.Andrea alisema DRC inaongoza kwa kuwa na radi nyingi na athari za radi hiyo, zimeikumba mikoa ya magharibi mwa Tanzania ya Geita, Kigoma, Kagera na Rukwa ambayo mara kwa mara inakumbwa na matukio ya radi. Alifafanua kuwa radi ni janga la asili ambalo ni tukio la cheche kubwa kutoka angani ambayo huwa na nguvu na huachiliwa kwa umeme na hutokea kutokana na tofauti ya nguvu za umeme kati ya mawingu na ardhi. | 3 |
MKUU wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka ametembelea Taasisi ya Utafi ti wa Kilimo (TARI) Kituo cha Uyole kilichopo Mbeya, kuona uzalishaji wa miche ya parachichi, kujifunza kilimo hicho na kuagiza miche bora 3,000 ili akapande mkoani humo.Ziara hiyo ni kutokana na taarifa zilizokuwa zikiripotiwa na vyombo vya habari kuhusu manufaa na faida kwa wakulima wa zao hilo. Mkuu wa Kituo cha TARI Uyole, Dk Tulole Bucheyeki alisema hayo alipokuwa akizungumza na HabariLeo wakati akikaribisha Mwaka Mpya 2020.Dk Bucheyeki alisema katika ziara hiyo, Sendeka alijifunza jinsi ya kupanda parachichi, mbolea inayotumika, matumizi ya viuatilifu na jinsi ya kupata masoko. Alishauri wananchi kupanda zao hilo, kwa kuwa soko lake ni kubwa ndani na nje ya nchi, kwani mti ukizalishwa kitaalamu unaweza kuzaa matunda 800 hadi 12,000 kwa mwaka.“Ekari moja unapanda miti 72. Ukichukua matunda 1,200 kwa mti kwa mwaka unapata matunda 86,400. Bei ya chini ya tunda moja la parachichi ni Sh 200. Ukiuza matunda hayo kwa ekari moja utapata zaidi ya Sh milioni 17. Ukiuza kwa eka 10 kwa mwaka utapata zaidi ya shilingi milioni 170 kwa mwaka.“Zao hili linaweza likastawi mahali popote pale nchini, inategemea ni aina ipi itakayopandwa katika sehemu husika,” alisema.Ofisa Uhaulishaji kituoni hapo, Rehema Olesenga alisema soko la parachichi lililopo hivi sasa, limehamasisha wakulima kupanda zao hilo, kwani awali kabla ya kuwepo kwa masoko rasmi yenye tija, wakulima walikuwa wakilisha nguruwe parachichi, ambayo mengi yalikuwa ni ya kienyeji, hususani katika eneo la Tukuyu mkoani Mbeya.Alisema kuwepo kwa masoko hayo kwa sasa, kumeleta hamasa kwa wakulima kwa kuongeza uzalishaji huo wa parachichi. Alitoa angalizo kuwa kuna wafanyabiashara waliojitokeza ambao sasa wameanza kuingilia parachichi, kwa kuvuna matunda machanga ambayo hayajakomaa, hivyo ni vema wakadhibitiwa mapema ili wasiliharibu soko hilo. Mtafiti wa Matunda kituoni hapo, Daud Mbongo alitaja aina za parachichi zilizopo kituoni hapo kuwa ni Hass, Fuerte, Ikulu, Booth 7, Weiso, Pinkerton na Simonds.Mbongo alisema aina ya Hass ina soko kubwa ndani na nje ya nchi na kwamba mnunuaji kabla ya kununua, huangalia ubora wa tunda kwanza. Pia aina ya Fuerte nayo ina soko nje ya nchi pia, lakini ni nzuri kwa soko la ndani.Mkurugenzi Mkuu wa TARI, Dk Geoffrey Mkamilo alisema taasisi hiyo inajihusisha na usambazaji wa teknolojia katika kuwafikia wakulima na wadau wengine wa kilimo. Alisema taasisi hiyo ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Namba 10 ya mwaka 2016 yenye jukumu la kutafiti, kusimamia na kuhamasisha matumizi ya teknolojia mbalimbali kwa wakulima na wadau wengine, ikiwemo kuratibu shughuli zote za utafiti wa kilimo Tanzania Bara.Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TARI, Dk Yohana Budeba alisema bila utafiti, maendeleo ya kilimo hayawezi kupatikana> Alisema utafiti ni gharama na unahitaji fedha nyingi. | 3 |
Mbunge wa CCM jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi ameishauri Serikali kuchukua hatua sawa na zinazochukuliwa na nchi nyingine sanjari na kujiweka karibu na marafiki wanaoinufaisha nchini. Chumi alikuwa akizungumzi suala la baadhi ya nchi kufunga mipaka yake lakini Tanzania kuendelea kuruhusu watu kutoka nchi hizo kuendelea kuja na kuchukua mizigo kama kawaida ambapo amesema Serikali haina budi nayo kufunga. “Mkono utoao ndio upokeao, wenzetu wanataka sisi tuwe tunatoa tu, haina maana wenzetu leo magari yao yako mpaka Tandika na Ilula yanachukua nyanya lakini sisi maroli yamezuiliwa namanga, ” Cosato Chumi-Mbunge Mafinga Mjini Alitolea mfano wa uturuki ambayo imeomba mara kadhaa kujiunga na umoja wa ulaya bila mafaniko na baadaye ikaamua kuchukua njia yake na inaenda vizuri hivyo na Tanzania inapaswa kushirikiana na wale ambao wapo tayari kushirikiana nayo. aidha hivi karibuni kumekuwepo na habari za baadhi ya nchi kufunga mipaka au kuweka mashariti magumu kwa madereva wanaotoka Tanzania sababu ikiwa ni mwenendo wa ugonjwa wa virusi vya corona. "Mkono utoao ndio upokeao, wenzetu wanataka sisi tuwe tunatoa tu, haina maana wenzetu leo magari yao yako mpaka Tandika na Ilula yanachukua nyanya lakini sisi magari yetu wameyazuia" Cosato Chumi-Mbunge Mafinga Mjini #CloudsDigitalUpdates A post shared by Clouds TV 🇹🇿 (@cloudstv) on May 14, 2020 at 4:21am PDT | 5 |
*Safari ya Azam, Yanga yanukia * Tippo adai watafanya biashara na timu yoyote NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM RAFU mbaya aliyoicheza beki mahiri wa Simba, Hassan Kessy dhidi ya mchezaji wa Toto African, Edward Christopher, imemsababishia kutemwa kuitumikia timu yake hiyo hadi mwisho wa msimu huu. Kessy alimchezea rafu Christopher kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha kutolewa nje kwa kadi nyekundu, huku uongozi wa Simba ukimuongezea adhabu ya kukosa michezo yote iliyobaki katika Ligi Kuu Tanzania Bara. Mbali na kusimamishwa kwa mchezaji huyo, tayari kuna tetesi za kuikacha klabu hiyo na kujiunga na kati ya klabu ya matajiri wa Bongo, Azam au Watoto wa Jangwani, Yanga, licha ya tetesi hizo kutokuwekwa wazi. Inadaiwa timu hizo Azam na Yanga zilikuwa zinasubiri kumalizika kwa michezo yao ya kimataifa ya marudiano kati ya timu za Esperance na Kombe la Shirikisho na Al Ahly mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ili zianze mchakato wa kumnasa beki huyo ambaye mkataba wake unaisha mwezi Juni. Akizungumza na MTANZANIA jana, Kessy alisema bado uongozi haujampa taarifa zozote za kusimamishwa kwake. “Sijapewa taarifa yoyote, lakini kama wameamua kunipa adhabu sawa nitaitumikia kwa kuwa bado ni mchezaji wao na bado nina mkataba nao, ila nikimaliza mkataba wangu mwezi wa sita meneja wangu ataamua kama nitabaki au nitaondoka,” alisema. Kwa upande wa meneja wake Athuman Tippo, alisema wamepokea maamuzi ya uongozi huo kumsimamisha mchezaji wake na ataitumikia adhabu hiyo kama ilivyoamuliwa kwa kuwa ni mwajiriwa wao. “Ataitumikia adhabu yake hadi atakapomaliza mkataba, lakini bado tunaendelea kusubiri adhabu watakayompa Vicent Angban na wasipofanya hivyo tutaendelea na msimamo wetu wa kuchukua hatua zaidi, tutakaa na mwanasheria na kupanga nini tufanye baada ya kipa huyo kujichukulia sheria mkononi kumpiga Kessy,” alisema. Alisema hadi sasa bado hawajafanya mazungumzo na timu yoyote nyingine, lakini Kessy akimaliza mkataba wake atakuwa huru hivyo watafanya biashara na timu yoyote itakayomtaka. Kessy jana alitangazwa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara, kuwa atakosa michezo yote iliyobaki katika ligi, akieleza alionekana kucheza rafu mbaya ambayo ingeweza kumsababishia kifo mchezaji huyo wa Toto. “Kessy ameihujumu timu kwenye mchezo huo kwa rafu mbaya aliyoicheza, iliyosababisha kupewa kadi nyekundu kwani hakuwa na sababu ya kucheza vile alionekana kabisa ameinua mguu sijui ni makusudi au bahati mbaya, angeweza kumsababishia hata kifo Edward, hivyo tumeamua kumuongezea adhabu badala ya kukosa mechi mbili kwa kadi aliyopewa atazikosa mechi zote tano,” alisema. Hata hivyo, mchezaji huyo mbali ya kucheza rafu hiyo iliyomuondoa Simba, alikuwa anaandamwa na jinamizi la kutoaminika tena Simba tangu alipoigharimu klabu yake katika mechi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kati ya Simba na Yanga iliyochezwa Februari 20 kwa kuokoa mpira kizembe ambao ulinaswa na mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma na kufunga bao kirahisi. | 4 |
['Wachezaji wa Barcelona wako tayari kuchelewa kulipwa mshahara ikiwa hatua hiyo itasaidia klabu klabu hiyo kumsajili tena mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil Neymar msimu wa joto, anasema beki, Gerard Pique.', "Barcelona ilifanya kila ''liwezekanalo katika uwezo wake'' kumsajili nyota huyo wa kimataifa lakini juhudi hizo ziligonga mwamba.", 'Neymar aliondoka Barcelona na kujiunga na Paris St-Germain kwa ada ya kuvunja rekodi duniani ya euro milioni 222 sawa na (£200m) mwaka 2017.', 'Pique alisema wachezaji wenzake waliiambia klabu hiyo kuwa wako tayari kuchelewa kulipwa mshahara ili kuisadia kufikia kanuni ya klabu ya malipo sawa ya wachezaji.', '"Tuko tayari kandarasi zetu zifanyiwe marekebisho," Pique alikimbia kituo cha radio cha Cadena Ser cha Uhispania.', '"Hutuna mpango wa kuchanga pesa, lakini tutarahisisha mambo kwa kuruhusu baadhi ya malipo kutekelezwa katika mwaka wa pili au watatu badala ya mwaka wa kwanza."', 'Barcelona ilitumia zaidi ya £200m msimu wa joto, katika usajili wa wachezaji kama Frenkie de Jong, kiungo wa kati kutoka Ajax na Antoine Griezmann kutoka Atletico Madrid.', 'Kanuni ya malipo sawa ya wachezaji, ambayo inazuia vilabu kutumia fedha kuliko uwezo wao, inasadikiwa kuwa moja ya suala ambalo Barcelona inatakiwa kushughulikia kabla ya kumsaini Neymar.'] | 4 |
JESHI la Magereza nchini limetakiwa kuleta mabadiliko ya kiutendaji, yatakayozingatia ubunifu na weledi wa kutumia rasilimali zao ili kuongeza uzalishaji mali, ukiwemo wa chakula kitakachojitosheleza kwa wafungwa na kupata ziada ili liondokane na kunyooshewa kidole.Agizo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Jacob Kingu.Alisema hayo juzi alipofungua kikao kazi cha wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara, kinachofanyika kwenye Ukumbi wa Magereza mkoani Morogoro.Alisema wizara imeunda Bodi ya Uzalishaji Mali ya Jeshi la Magereza, ambayo ina wataalamu mbali mbali wenye uzoefu wakiwemo wastaafu itakayokuwa na jukumu la ufuatiliaji mzuri wa shughuli za uzalishaji mali wenye kuleta tija ndani ya jeshi na Taifa kwa ujumla.Alisema eneo la uzalishaji mali hasa kwenye kilimo ni lazima kuwepo na mabadiliko na si kutegemea kilimo cha mvua pekee, ni vyema likatenga maeneo maalumu kwa kilimo cha umwagiliaji na jambo hilo linawezekana.“Kupanga ni kuchagua... lazima sasa kuwepo na mabadiliko, kuwepo na mpango mkakati wa muda mfupi, muda wakati na muda mrefu kwenye kilimo cha umwagiliaji kwa kuchimba visima virefu vya umwagiliaji na kisima kimoja hakizidi shilingi milioni 20,” alisema Meja Jenerali Kingu.Alisema jeshi hilo lina uwezo mkubwa katika kuongeza uzalishaji wa chakula na hata mapato ya ndani, iwapo likitumia vyema rasilimali zake na kuweka malengo shindanishi kwa Magereza na hilo litawezesha kuleta mabadiliko makubwa na hivyo kuondokana kwenye kunyooshewa kidole.Pia, alilitaka kuimarisha Kitengo cha Ujenzi ili kutumike vyema kujenga nyumba za maofisa na askari kwa kuwa lina nguvu kazi ya kutosha na kinachohitajika ni kuwatambua wataalamu walipo ili watumie taaluma zao.“Ni vyema Kikosi cha Ujenzi cha Jeshi kiimarishwe kiwe cha ushindani, lazima kuleta mabadiliko kwenye sekta ya ujenzi ambayo ina kuwa kila leo na ufanyike uhakiki wa wataalamu mlionao ili waweze kutumika kwenye kazi hizi walete mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza,” alisema Meja Jenerali Kingu.Alilipongeza jeshi hilo kwa kujenga majengo ya ofisi tatu za wizara katika Mji wa Serikali jijini Dodoma ; na hatua hiyo ni chachu ya kuliwezesha kupata fursa nyingine za zabuni za ujenzi wa nyumba za serikali na za wananchi.Aidha, alilitaka kutumia vyema ardhi iliyopo na kuwa na hati miliki ikiwa na kuyaendeleza kwa kilimo cha mazao ya aina mbali mbali, upandaji wa miti ya mbao na matunda kwa lengo la kuondokana na maneno kuwa sehemu ya ardhi yao haitumiki vizuri. | 3 |
NCHI wanachama Jumuiya wa Afrika Mashariki (EAC) zimethibitisha kushiriki kwa pamoja kwenye mradi wa wanawake wajasiriamali milioni 50 wa Afrika, unaolenga kuwawezesha wanawake kiuchumi.Mradi huo unaotarajiwa kumalizika Desemba 2020, utafadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) na utakuwa unapatikana kupitia mifumo ya kielektroniki kama vile simu na kompyuta.Aidha, wanawake wa Tanzania na nchi zingine za Afrika Mashariki, watapata fursa ya kufahamu mahali fursa zilipo, mafunzo ya kibiashara na masoko ya bidhaa zao.Naibu Katibu Mkuu wa EAC, Christopher Bazivamo amesema Dar es Salaam kuwa mradi huo ni mradi rafiki na wenye maslahi mapana kwa watu wa Afrika Mashariki. Alisema nchi za Afrika Mashariki hazina budi kushirikiana kwenye biashara.Alisema, “Fursa hii kwenye mradi wa 50 Million African Women Speak Networking, umelenga kuwapa wanawake mitaji, masoko na mafunzo yenye lengo la kuwainua kiuchumi.Ofisa Maendeleo Mwandamizi, Idara ya Jinsia ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, John Mapunda alisema wajasiriamali wataunganishwa kupitia mradi huo unaolenga wanawake milioni 50.Alisema ni mradi ambao unatekelezwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki, pia katika nchi za Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Magharibi mwa Afrika (ECOWAS) na Soko la Pamoja la Nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na lengo lake kubwa ni kuwawezesha wanawake kiuchumi na hususani wanawake wajasiriamali.“Kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mradi unatekelezwa kwenye nchi sita. Na sio jumuiya ya Afrika Mashariki tu bali hata katika nchi nyingine nje,” alieleza Mapunda.“Sasa kwa maana ya taarifa za fedha tunamaanisha taarifa kwa mfano za wapi mikopo inapatikana, wapi fursa zinapatikana lakini ili waweze kutumia kama mitaji kuendesha biashara. Pia kutakuwa na taarifa ambazo sio za fedha kama vile za mafunzo,” alisema Mapunda.Pia alisema taarifa zinazohusu masoko na mambo mengine ya kutambua thamani na wapi kwenye uhitaji na hata usalama wa biashara, kwani kuna baadhi ya nchi nyakati za uchaguzi hakuko salama, hivyo lazima wajasiriamali hao wawe na taarifa.Alisisitiza kwamba lengo kubwa la mradi huo ni kuhakikisha ni namna gani taarifa hizo, zitawafikia wanawake wajasiriamali na ndio maana matarajio ni kuandaliwa kwa tovuti, ambayo ndani yake kutakuwa kunawekwa taarifa zote muhimu.Alifafanua kuwa wameona kuwa wanaweza kutengeneza tovuti nzuri na kuweka taarifa zote lakini kama wanawake wajasiriamali.Hivyo, alisema ni fursa muhimu kwao kukutana na vyombo vya habari, kwani kwa kutumia njia zao za kufikisha taarifa watawafikishia wanawake wajasiriamali taarifa za mradi huo na wanafanya hivyo kwa kuamini kuna takribani ya wanawake milioni 500. Malengo ni kuwafikia wanawake asilimia 10, ambayo ukiiigiwa unapata wajasiriamali milioni 50 kwa jumuiya tatu ambazo kuna nchi 38. | 5 |
JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahimu Juma amewataka majaji na mahakimu kuepuka kuruhusu ndugu na marafi ki zao kuwatumia kama milango ya kuvunja sheria kwa namna yoyote au kujinufaisha.Aidha, aliwataka kulegeza masharti ya dhamana kwa raia wa Tanzania, kwa sababu wana haki ya kupata dhamana na kwamba wanapaswa kuwaamini wanapotumia vitambulisho vyao.Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuapisha Naibu Wasajili wa Mahakama na kuwakabidhi vitendea kazi mahakimu wafawidhi. Jaji Juma alisema wapo baadhi ya ndugu wa majaji au mahakimu wanaovunja sheria kwa kuchukua mali za watu wengine kwa kupitia vyeo vya ndugu zao.“Unakuta mke wa Jaji au Hakimu anatumia nafasi ya mume wake kuliko Hakimu au Jaji mwenyewe mpaka anaogopeka katika jamii. Wengine wanachukua mali za wengine na kuvunja sheria, hii si sawa kabisa, kazi yenu si kuwa mawakili wa familia au watoa msaada wa kisheria bali ni kutoa haki,” alisema.Aliwataka wasitumie nafasi walizonazo kuzungumza na wakuu wa vituo vya polisi kwa ajili ya kuondoa mashitaka kwa ndugu zao, badala yake wahakikishe wanafuata sheria kwani hakuna mtu aliyejuu ya sheria. Kadhalika, aliwataka mahakimu kutokubali kuahirisha mashauri kwa hoja nyepesi zinazotolewa na waendesha mashitaka kwamba upelelezi wa kesi unaendelea na kuwa ni lazima mahakimu watumie nafasi yao kuwabana waendesha mashitaka ili waseme ni upelelezi gani unaofanywa ambao haukamiliki kwani ndio chanzo cha kutomaliza mashauri kwa wakati.“Msikubali waendesha mashitaka wawatishe kwa jambo lolote akifanya hivyo mpeleke kwa mtendaji kwa sababu kitendo hicho ni kukiuka maadili. Pitieni mabadiliko mbalimbali ya sheria ambayo yatatusaidia kumaliza kesi kwa wakati,” alisisitiza.Kuhusu dhamana, Jaji Juma alisema mahakimu wasiwe wagumu kutoa dhamana kwa Watanzania, kwa sababu ni haki yao na wasizuie kwa matakwa yao binafsi. Alieleza kuwa mshitakiwa atakuwa na wadhamini wenye vitambulisho vya uraia wapewe dhamana na endapo atakimbia maana yake atajihukumu kwa kukimbia uraia wake.Akizungumzia sheria ya makubaliano, Jaji Mkuu alisema sheria hiyo imekataza makosa machache na kwamba haitumiki kwa mashitaka ya utakatishaji fedha na uhujumu uchumi pekee na kufafanua zaidi kuwa sheria hiyo ambayo mshitakiwa anaingia makubaliano na Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), inapaswa kutumika kwa makosa mengi zaidi kwani anaamini itasaidia kupunguza msongamano gerezani.Manaibu Wasajili walioapishwa ni Happiness Ndesamburo, Warsha Ng’humbu, Elizabeth Nyembele, Niku Mwakatobe, Arnold Kirekiano, David Ngunyale, Flora Mtarania, James Kareyamaha, Magdalena Ntandu, Chiganga Tengwa na Godfrey Isaya. Mahakimu Wafawidhi waliokabidhiwa vitendea kazi ni Hassan Makube, Gadieli Mariki, Ebiseeza Kalegeya, Maira Kasonde, Martha Mahumbuga, Elimo Massawe, Silvia Lushashi, Monica Ndyekobora, Gabriel Ngaeje na Venance Mlingi. | 3 |
VINARA wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, Azam FC wamepata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo dhidi ya maafande wa JKT Tanzania uliochezwa kwenye uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo,jana.Bao la Azam lilifungwa dakika ya 52 na Yahya Zayd baada ya kupata krosi nzuri ya mshambuliaji Donald Ngoma. Azam FC ilicheza pungufu ikiwa na wachezaji 10 kuanzia dakika ya 36 baada ya mchezaji Enock Atta kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kumfanyia madhambi mchezaji wa JKT.Huo ni mchezo wa kwanza kwa JKT kupoteza tangu kuanza kwa msimu huu mbele ya Azam wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani, huku wageni hao wa Chamazi wakiendelea kukaa kileleni kwa pointi 24 pasipo kupoteza mchezo wowote.Awali, timu zote mbili ziliingia kwa kasi na kila mmoja akionekana amejipanga vizuri katika safu ya ushambuliaji na ulinzi, wote walicheza mchezo wa nguvu lakini baada ya kadi nyekundu Azam walishuka kidogo ingawa waliongoza kwa kumiliki mpira.Hadi kipindi cha kwanza kinamaliza timu hizo hazikuwa zimefungana, lakini kipindi cha pili Azam ilikuja kwa nguvu tena na kuwazidi kete wapinzani wao kwa kufanya shambulizi la kushtukiza na kupata bao hilo la ushindi lililodumu hadi mpira ulipomalizika.Kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, Alexander Sanga anaripoti kuwa Mbao ilishindwa kutamba nyumbani na kukubali kipigo cha mabao 3-1 dhidi ya Lipuli. Ni mara ya kwanza Mbao kupata kipigo kikubwa ikiwa kwenye uwanja huo kwani wengi wanaokwenda hapo hawatoki salama.Aidha, Ruvu Shooting ilitoa kipigo cha mabao 3-0 dhidi ya Singida United kwenye uwanja wake wa Mabatini, Mlandizi. Pia, Prisons walitoka suluhu dhidi ya African Lyon, matokeo ambayo sio mazuri kwa timu zote mbili kulingana na nafasi walizopo.Kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga wenyeji Coastal Union walilazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Kagera Sugar. Kagera imeendelea kulinda nafasi yake ya kutopoteza mchezo wowote tangu kuanza kwa msimu huu, ikiongeza idadi ya mechi za sare. | 4 |
JANETH MUSHI-ARUSHA KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan Shanna, amesema jeshi hilo kwa kushirikiana na kikosi kazi cha ujangili Kanda ya Ziwa, wamekamata watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na bunduki ya kivita aina ya AK 47 na risasi 12. Alisema watuhumiwa hao ambao majina yao yamehifadhiwa walikamatwa Mei 10 mwaka huu saa saba mchana. Alisema watuhumiwa hao walikamatwa katika Kitongoji cha Oloshoo, Kata ya Enguserosambu wilayani Ngorongoro Mkoa wa Arusha. Alisema bunduki hiyo ilipatikana baada ya kikosi hicho kupata taarifa fiche kuwa kuna watu wanne, wawili Watanzania na wawili Wakenya wameonekana maeneo ya mpakani wakiwa wanajipanga kuwinda wanyama katika moja ya mbuga zilizopo nchini. “Tulifanya msako ambao ulifanikisha kupatikana kwa bunduki moja ya kivita na risasi 12. Wanasadikiwa walikuwa na bunduki mbili za kivita, wengine wamekimbilia Kenya. “Jeshi la Polisi linawataka wahalifu hao kujisalimisha kituo chochote cha polisi kwani wasipofanya hivyo tutalazimika kutumia nguvu kubwa kuwatafuta ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. “Nitumie fursa hii kuwashukuru wananchi wanaoendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu, nawaomba waendelee kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuwafichua wale wenye nia ovu ili kumaliza uhalifu katika mkoa wetu,”alisema | 3 |
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umekanusha taarifa zisizo rasmi kuhusu kuwepo kwa viwango vipya vya michango ya uanachama katika kupatiwa huduma za afya.Hata hivyo ilibainishwa jana kuwa upo mchakato wa kuunda vifurushi tofauti vya uchangiaji kwa makundi tofauti ya uanachama ili kuwezesha watu kujiunga kulingana na uhitaji wao. Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi ya uhusiano, taarifa zinazosambaa sio rasmi kwa hiyo zipuuzwe. Ilieleza kuwa mfuko umeanzisha vifurushi vya makundi mbalimbali ya wanufaika kama waajiriwa, watoto, wakulima na hata wajasiriamali. Kuhusu taarifa rasmi ikoje katika eneo hilo la kuongeza viwango vipya vya uchangiaji, Ofisa Mahusiano na Elimu kwa Umma, wa NHIF, Grace Kisinga alisema taarifa ya mfuko kuhusu suala hilo ndivyo ilivyo na kwamba wanachama wanachangia kwa taratibu zilizopo.Kuhusu kuongeza wigo wa wanufaika, alisema ili kuongeza wanufaika, mfuko pia ulishaanza mchakato wa kuunda vifurushi tofauti vya uchangiaji kwa makundi tofauti ya uanachama ili kuwezesha watu kujiunga kulingana na uhitaji wao. Alisema mchakato huo upo katika hatua za kukamilika katika ngazi mbalimbali za uongozi na utakapokamilika taarifa rasmi zitatolewa na mfuko wa umma. Iliongeza kuwa kwa sasa Mfuko unaendelea kusajili wanachama kupitia taratibu zilizopo za uchangiaji..Hata hivyo, NHIF, iliomba radhi kwa usumbufu wowote uliosababishwa na taarifa hizo zisizo rasmi na kuendelea kuwahimiza wananchi kufuatilia taarifa za NHFI kupitia tovuti yake. Wakati huo huo, kupitia tovuti ya mfuko huo, umeanza utaratibu wa uhakiki wa wanachama waliosajiliwakwa kwa wastaafu ili kuhuisha taarifa na kuweka kumbukumbu sahihi tangu Januari Mosi ukitarajiwa kukamilika Machi 30, mwaka huu.Ilielezwa kuwa kazi ya uhakiki unawahusu wanachama wastaafu walioandikishwa katika mfuko huo kuanzia Julai 2009 hadi Septemba 2018. Ilieleza kuwa uhakiki huo unafanywa kwa ofisi zote NHIF zilizopo Tanzania bara na Ofisi za Zanzibar. Mwanachama mstaafu atahitajika kufika katika ofisi yoyote ya NHIF akiambatana na mwenza wake (endapo yupo) na iwapo mwanachama mstaafu amefariki, mwenza aliyebaki atatakiwa kufika katika ofisi za mfuko huo kwa ajili ya uhakiki.Aidha mstaafu huyo atatakiwa kufika katika uhakiki huo akiwa na vitambulisho vya NHIF, cheti cha ndoa (mstaafu mwenye mwenza), na kitambulisho cha uraia, mpiga kura, leseni ya gari au hati ya kusafiria. Iliongeza kuwa wanachama wastaafu wanahimizwa kufuatilia taarifa hiyo na muda uliowekwa ili kuepuka usumbufu wakati wa kupatiwa huduma za afya. | 3 |
KAMPUNI ya Vodacom Tanzania imeongeza ushiriki wa wasichana katika masuala ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM), kupitia mafunzo ya teknolojia ya ku-code yaliyodhaminiwa na kampuni hiyo.Awamu ya pili ya mafunzo hayo ilichukua siku tano na kushuhudia wanafunzi 59 wakihitimu mafunzo yaliyofanyika katika Taasisi ya Dar Teknohama Business Incubator (DTBI).Shirika la Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) linasema, ‘ushiriki wa wanawake katika sayansi na teknolojia ni mdogo ukilinganisha na wanaume.Code like a girl ni programu ya kimataifa yenye lengo la kuandaa wasichana kuwa na ujuzi unaohitajika katika soko la ajira ya tekinolojia.Vodacom imesema, kwa kushirikiana na DTBI, mafunzo hayo yalijumuisha elimu ya lugha za kompyuta na utengenezaji wa programu kama HTML, CSS, GitHub and Bootstrap.Mafunzo yalitolewa kwa mfumo wa ushirikiano na yalijumuisha mafunzo ya kijamii na ku-code kuwawezesha kutengeneza tovuti. Washiriki pia walipata mafunzo kuwasilisha mada na mawasiliano.“Tumefurahishwa na wanafunzi waliohudhuria semina hii, wiki ilifana na mafunzo mbalimbali ya maisha, coding, mawasilisho, na mafunzo ya ujuzi wa mawasiliano, “ ilisema Vodacom.“Wasichana walikuwa wamiliki wa tovuti ambazo walitengeneza wao “ alisema Zaituni Ally, Mkuu wa Kitengo cha Ufanisi wa Shirika akimwakilisha Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Vodacom, Vivienne Penessis na kuongeza:“Mabadiliko ya kidijitali yanatokea kila mahali duniani, hivyo ni muhimu kuandaa wasichana kwa mabadiliko haya katika soko la ajira”.Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTBI Dk George Mulamula alisema; “awamu ya kwanza ya mafunzo, tuliona idadi kubwa ya wanafunzi, hasa wasichana katika shule za sekondari wanafundishwa kwa nadharia badala ya vitendo kuhusiana na teknolojia ya Mawasiliano (ICT).“Hivyo basi mkakati huu wa mafunzo haya una lengo la kuwawezesha wasichana nchini kote kupata elimu ya ICT, kuwasaidia kupata fursa mbalimbali katika mazingira ya teknolojia kama vile vijana wenzao wa kiume, “ aliongeza.Lengo la Vodacom ni kutoa fursa wasichana nchini kote kushiriki a masomo ya STEM; “Coding ndio nati na spana za dijitali siku zijazo. Kupitia mipango kama hii, tunatarajia kuona wasichana wengi katika Teknolojia. Pia kuwasaidia vijana kupanua ujuzi wao kupitia teknolojia kuleta maendeleo, “alielezea Zaituni. | 3 |
BALOZI wa Tanzania nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Luten Jenerali Mstaafu Paul Mella amesema licha ya kikosi cha Simba kupoteza mchezo wa dhidi ya As Vita, bado wana nafasi ya kufanya vizuri kwenye michezo iliyobaki ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika Kundi D.Alisema kitendo cha kupoteza mchezo huo wa ugenini wamepata funzo kubwa la kujitathimini kwenye kikosi hicho na kujipanga upya ili kuhakikisha wanapata matokeo mazuri yatakayo wafanya kusonga mbele.Mchezo huo wa hatua ya makundi katika Ligi ya Mabingwa Afrika ulipigwa juzi, ambapo wawakilishi hao pekee nchini katika mashindano ya soka ya Kimataifa, walipoteza mchezo kwa kukubali kichapo cha mabao 5-0.Akizungumza juzi wakati anakiaga kikosi cha timu hiyo tayari kwa kurejea nyumbani, Mella aliwatia moyo wachezaji wa timu hiyo nakwamba bado wananafasi ya kufanya vizuri kwa kuwa timu hiyo inakikosi kizuri kama wachezaji watajituma watafuzu na kusonga mbele.“Licha Simba kupoteza mchezo huo dhidi ya As Vita Club. Naamini wanakikosi kizuri ambacho kinauwezo wa kufanya vizuri michezo inayokuja na kufuzu kwenye hatua inayofuata kikubwa ni kuongeza juhudi ya kujituma na kujipanga kwa kufanya maboresho yaliyojitokeza, “ amesema Mella.Mwenyekiti wa Simba Swedi Mkwabi amesema walikutana na kisiki na hakika wamejifunza mengi kupitia mchezo huo na kuahidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza ili kuhakikisha wanafanya vizuri katika michezo iliyobaki.“Kundi letu lina ushindani kila timu ina nafasi ya kufanya vizuri ndio maana kila timu inafanya vizuri kwenye michezo yao ya nyumbani tunarudi tunaenda kujipanga kwa mchezo dhidi ya washindi wa pili wa mashindano hayo, Al Ahly ya Misri kuhakikisha tunapata matokeo mazuri,” amesema.Naye mchezaji zamani wa timu hiyo, Mtemi Ramadhan amewsema mpira wa siku hizi unatakiwa uchezwe kama ukiwa darasani, kama unajua mchezo unaenda kupoteza unatakiwa utumie mbinu ya kujilinda kocha alienda katika mchezo huo kwa lengo la kushambulia na ndio maana wakufungwa.“ Bado wananafasi ya kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza na matumaini yangu kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa hapa nyumbani, watashinda, ” amesema Mtemi.Simba ipo kwenye Kundi D, ambalo hadi sasa Al Ahly wanashika usukani kwa kuwa na pointi nne wakifunga mabao matatu huku AS Vita Club ikishika nmafasi ya pili wakati Simba iliyoanza kwa kuongoza kundi, sasa iko nafasi ya tatu.Katika mchezo wa kwanza, Simba iliuanza michuano hiyo kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya JS Soura ya Algeria kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, ambao wana pointi moja hadi sasa. | 4 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.