text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
KATIKA kuboresha huduma za maji, Benki ya Dunia (WB) imeipa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Sh milioni 77 ikiwa ni malipo ya miradi ya ufanisi.Hayo yalisemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Rebman Ganshonga wakati wa kikao cha baraza la Madiwani kupitia taarifa za Kata. Alisema kuwa kwenye bajeti iliyopita Halmashauri ilipokea Sh milioni 33 ikiwa sehemu ya mradi wa malipo ya ufanisi katika miradi ya maji na kuongeza kuwa fedha hizo zimelenga katika kufungua vituo vipya vya kutoa huduma ya maji katika Kata ya Dutumi, Kikongo na katika kata nyingine za halmashauri ya wilaya ya Kibaha vijijini.“Tumefanya vizuri katika miradi ya malipo kwa ufanisi ndiyo sababu ya kuongezewa fedha ambazo zitasaidi uboreshaji huduma za maji,”alisema Ganshonga. Alisema licha ya baadhi ya changamoto za huduma za maji, halmashauri imejipanga kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.Diwani wa Kata ya Dutumi, Mkali Kanusu alisema Kata yake imepokea Sh milioni 13 kwa ya malipo ya ufanisi na kwamba wamezitumia fedha hizo katika uboreshaji miundombinu ya maji. Kanusu alisema wamekuwa wakipata changamoto kubwa ya maji ikifika katika msimu wa kiangazi kutokana na kupungua kwa kina cha maji katika chanzo wanachokitegemea kwenye Mto Ruvu.Alisema wanaipongeza Benki ya Dunia kwa kuwapatia fedha hizo kwani itawasaidia kukabili changamoto ya maji. “Lengo ni kuhakikisha maji yanapatikana kwa uhakika na wananchi wanaondokana na adha hiyo,”alisema Kanusu. | 3 |
MHADHIRI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kutoka Idara ya Sayansi ya bahari na teknolojia ya uvuvi, Samwel Limbu kwa miaka miwili ya masomo nchini China, amekuwa mwanafunzi bora wa kimataifa katika Chuo cha East China Normal University (ECNU).Limbu amekuwa mwanafunzi bora wa kimataifa kwa mwaka wa masomo 2015/16 na 2017/18. Taarifa iliyotolewa na Ofisa Uhusiano wa UDSM, Isdory Jackson ilisema hata serikali ya China inatambua ubora huo wa kimataifa kwa mwaka wa masomo 2016/17.Limbu ambaye chuoni UDSM ni Mhadhiri katika ndaki ya sayansi za kilimo na teknolojia ameonyesha jitihada kwa kutoa makala za kitaaluma 11 ikiwemo ya shahada ya uzamivu iliyopata alama ya juu ya 7.3 pamoja na sura tatu tokea ameanza masomo ya uzamivu chuoni hapo.“Kupitia mwanafunzi huyo Limbu, chuo kikuu hicho cha China imekitambua Chuo Kikuu Dar es salaam kuwa ni kituo chao barani Afrika kwa ajili ya kuungana kwenye tafiti pamoja na maabara za kitaaluma,” ilisema taarifa hiyo.Kutokana na mafanikio hayo, taarifa inasema Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye pamoja na wanajamii wa chuo hicho wamempongeza Limbu kwa heshima kwa taifa lake pamoja na chuo Kikuu cha Dar es Salaam. | 3 |
Na AVELINE KITOMARY – DAR ES SALAAM SAFI wa vyoo ni muhimu kulinda afya ya binadamu na kuweka mazingira salama ambayo yanafanya jamii iweze kuepukana na magonjwa ya lipuko. Wapo watu ambao wanajihusisha kufanya kazi za usafi wa vyoo ‘maarufu kama vyura’ ikiwemo kuzi- bua vyoo vilivyoziba na kuhamisha majitaka kwa vyoo vilivyojaa. Kazi hiyo ina umuhimu mkubwa
kwa jamii na uwezekano wa vijana
kupata ajira ni mkubwa kwani baada
ya uzoaji wa majitaka pia yanaweza
kutumika kwa matumizi mbalimbali
kama mbolea, gesi na umwagiliaji.
Ingawa kazi hii ni muhimu lakini pia ni hatarishi hasa kwa wale wanaofanya bila kuwa na vitendea kazi sahihi. Wapo wafanyakazi wanaopoteza
maisha au hata kujeruhiwa kutokana
na mazingira mabaya ya utendaji kazi.
HALI ILIVYO
Ripoti zilizotolewa hivi karibuni
na Shirika la Wateraid kwa kush-
irikiana na Shirika la Afya Duniani
(WHO), Shirika la Kazi Duniani
(ILO) na Benki ya Dunia, zinasema
pamoja na kuimarika kwa huduma za
jamii katika nchi zinazoendelea, bado
wafanyakazi wa usafi vyooni wako
hatarini kuathirika kiafya.
Ripoti hiyo ilieleza kuwa India
pekee kati ya mwaka 2017 na 2018
watu watatu wanaofanya kazi hiyo
hufariki dunia kila baada ya siku tano,
huku kwa mwezi mmoja watu 18
wanapoteza maisha na kwa mwaka ni
watu 216.
Shirika la Water Aid Tanzania
limesema watu wanaojihusisha na
kazi za usafi vyooni wako hatarini
zaidi kupoteza maisha kutokana na
mazingira hatarishi.
Meneja Miradi Mwandamizi wa
Water Aid Tanzania, Twaha Mubarak,
anasema kuna haja ya kuwaangalia
wafanyakazi wa vyooni kwani wao
ndiyo wanahakikisha jamii inakuwa
katika mazingira salama kwa kufanya
usafi.
Anatoa wito kwa Serikali kuten-
geneza mazingira wezeshi na mfumo
rasmi kwa watu wanaofanya kazi za
usafi wa uzoaji taka wa vyoo.
“Katika suala la usafi, bado kuna watu hatujawatazama sawasawa, watu hawa ni wale wanaofanya kazi sekta ya usafi, hasa wale wanaohusika na uzoaji wa taka za vyooni hadi kutupa takataka. “Ripoti inabainisha mazingira mabaya ya mamilioni ya wafanyakazi ambao wanafanya kazi katika mazingira hatarishi kwa afya zao. “Pamoja na kuimarika kwa huduma
za jamii, kundi hili limekuwa likiach-
wa katika mazingira mabaya, hawana
vitendea kazi, lengo la ripoti ni kuinua
ufahamu kuhusu mazingira hatarishi
wanayopitia watu hawa wa mnyor-
oro wa usafi kama kusafisha vyoo,
kutapisha mashimo ya vyoo, kusafisha
mitaro na kusimamia njia ya kutibu
maji taka.
“Wafanyakazi hawa mara kwa
mara wanagusa vinyesi vya binadamu
wakiwa hawana vifaa vya kuwakinga,
hali hii inaweza kuwafanya kupata
magonjwa hatarishi.
“Ukiacha vifo, kuna wale wa-
naopata maumivu, ajali na magonjwa
ya mara kwa mara au yanayojirudia na
pia kuna ugonjwa kama kipindupindu
ni hatari,” anasema Mubarak.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Uhai
Mazingira na Watu (UMAWA),
Mathias Milinga, anaiomba Seri-
kali kuongeza nguvu katika kazi za
uchakataji wa maji taka ili kuongeza
ajira kwa vijana.
“Huwa tunakuwa na mfumo rasmi
wa kuchakata na kufanya uzalishaji
ambao utatumika kwa mahitaji ya bin-
adamu, ipo mitambo ambayo inatu-
mika, yale maji taka yanafaa kutengen-
ezea mbolea, mkaa wa kupikia, gesi na
pia maji masafi, kwa hiyo hii itasaidia
kutunza mazingira,” anasema Milinga.
KISA CHA CHISENGO
Julius Chisengo ni mkazi wa jiji
la Dar es Salaam na baba wa watoto
watano, kwa miaka 12 sasa amekuwa
akifanya kazi za usafi vyooni kama
kuhamisha majitaka na kuzibua vyoo.
Kutokana na kukaa kazini muda mrefu uwezo wake wa kufanya kazi hiyo sasa umekuwa mkubwa hata
uelewa umeongezeka pia.
Anasema kazi hiyo ndiyo inayom-
wingizia kipato na kulisha familia
yake hivyo ni muhimu kwake.
“Nina muda mrefu tangu nianze
kufanya kazi hii na naipenda kwa
sababu inanisaidia. Nasomesha wa-
toto, natunza familia hivyo nafaidika
japo ni kazi hatarishi pia,”anasema.
Chisengo anasema kazi hiyo pia
ilishawahi kumwathiri kiafya na kum-
sababishia ulemavu wa mguu.
“Changamoto kubwa niliyoipata
nilivunjika mguu wa kulia wakati
ule ambao sina elimu, mtu akiniita
kuzibua choo naenda tu sasa siku hiyo
nilikanyaga mti uliooza ukavunjika
nikaanguka na kupata ulemavu.
“Niliuguzwa kwa muda mrefu
hadi nilipopata nafuu, si unaona huu
mguu wangu mmoja (anamuonesha
mwandishi) haulingani na mwing-
ine japo najitahidi kusimama vizuri.
Huu ni kama ulemavu tu kwangu
lakini hata sasa namshukuru Mungu,”
anasema.
Anasema mazingira, kutokuwa na
vitendea kazi na upeo mdogo wa ujuzi
vilisababibisha akaumia.
“Kwasasa afadhali kuna tofauti ki-
dogo uelewa ninao nimepata mafunzo
mengi na ninapokwenda kazini naan-
galia kwanza usalama na vitendea kazi
nitakavyotumia,” anasema.
Anasema wafanyakazi wenzake wawili pia waliwahi kuumia na wote sasa wana ulemavu wa miguu. “Hizi kazi zinahitaji vifaa, usipoku-
wa na ujuzi kuumia ni rahisi kwa
sababu kila kifaa kina sehemu yake.
“Wakati nafanya kazi kuna marafiki
zangu wawili walipata ajali na kuumia
na sasa ni walemavu wa miguu,”
anasema.
Chisengo anatoa wito kwa serikali kuangalia kazi hizo kwani ni sehemu
muhimu ya afya ya jamii.
“Tunafanya kazi ya kulinda afya ya
jamii, sisi tunasaidia kukabiliana na
magonjwa ya mlipuko kama kipin-
dupindu na mengine.
“Naomba Serikali watutengenezee
mfumo rasmi na watoe elimu maeneo
yote ili watu wajue kazi hii inahitaji
nini,” anasema Chisengo.
MAJITAKA NI DHAHABU
Tekonlojia inaweza kubadilisha ma-
jitaka hasa ya vyooni kwa matumizi
mengine.
Meneja Miradi Ufuatiliaji Tathimini
na Ripoti kutoka Shirika la Wateraid,
Reginald Kwizela, anasema wana-
tumia majitaka kutengeneza maji
kwa ajili ya umwagiliaji na gesi kwa
matumizi ya nyumbani.
“Tukishachukua majitaka kutoka
kwa mteja huwa tunayaleta kwenye
kituo ambacho kina sehemu ya kum-
waga.
“Unapomwaga pale maji yanain-
gia kwenye shimo kubwa ambalo
limejengwa kwa tofali halivuji na
kuna sehemu yatakapofikia yanaha-
mia upande wa chemba nyingine
yanachujwa tope linabaki chini maji
yanapanda juu.
“Unapomimina pale kuna
bomba limeenda mpaka chini
kwa hiyo maji yanahamia chemba
ya pili, ya tatu zipo tisa sasa hiyo
ya tisa ukioneshwa kuwa haya ni
majitaka huwezi kuamini. Ni me-
upe hayana hata harufu yakifika
sehemu ya 10 yanaenda kwenye
bwawa kwa ajili ya kumwagilia
shamba.
“Gesi inatokana na tope kuna
bomba limeenda moja kwa
moja mpaka kwenye nyumba ya
makazi, gesi hii inatumika kwa
ajili ya kupikia,” anasema.
Anasema baada ya miezi mi-
tatu tope likikauka huchukuliwa
na kuwekwa sehemu nyingine
tayari kutumika kama mbolea.
| 0 |
BARCELONA, HISPANIA WASHAMBULIAJI hatari wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar, wamefanikiwa kufikisha mabao 300 tangu watatu hao walipoanza kucheza pamoja ndani ya klabu hiyo. Juzi klabu hiyo ilishuka dimbani katika mchezo wa Copa del Rey dhidi ya wapinzani wao Athletic Bilbao, ambapo Barcelona imefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali baada ya kushinda mabao 3-1 na kuifanya iwe na jumla ya mabao 4-3, baada ya mchezo wao wa awali Athletic Bilbao ikishinda mabao 2-1. Mabao hayo ya Barcelona yalifungwa na nyota hao watatu, huku bao la Athletic Bilbao likifungwa na nyota wao, Enric Saborit, lakini kwa upande wa nyota hao wa Barcelona wameweka historia ya kuwa na jumla ya mabao 300 baada ya kila mmoja kufunga katika mchezo huo wa juzi. Wakati huo nyota wa Barcelona, Messi, amefikisha jumla ya mabao 31 ya kupigwa kwa mpira wa adhabu tangu kuanza kwa soka lake la kimataifa, wakati huo bao lake la juzi la mpira wa adhabu likiwa la 26 na kufikia rekodi ya kocha wa sasa wa klabu ya Everton, Ronald Koeman, ambaye alifunga wakati akiwa mchezaji. Kocha huyo wa Everton wakati anacheza soka alikuwa anacheza nafasi ya kiungo na wakati mwingine alikuwa anacheza nafasi ya ulinzi, lakini tangu anaanza soka hadi anastaafu alicheza jumla ya michezo 613 ya klabu na timu ya taifa huku akifunga jumla ya mabao 207. Koeman kupitia akaunti yake ya Instagram, haraka alimpongeza Messi kwa kufikia rekodi yake ya mabao 26 ya mipira ya adhabu. “Hongera sana Messi kwa kufikisha mabao 26 ya mipira ya adhabu, ninaamini rekodi hiyo utaivunja,” aliandika Koeman. Kwa upande mwingine bao ambalo lilifungwa na Suarez, lilimfanya afikishe bao lake la 100 tangu ajiunge na klabu hiyo mwaka 2014 akitokea timu ya Liverpool ya nchini England. | 4 |
MAOFISA wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wamefanikiwa kumkamata muagizaji wa jumla wa nguo za ndani za mitumba zilizopigwa marufuku kutumika nchini kwa mujibu wa Sheria ya Viwango namba 2 ya mwaka 2009. Kukamatwa kwake ni mafanikio makubwa kwa maofisa wa TBS kwani kupitia msako huo, wengi waliokamatwa ni wachuuzi wadogo kutoka kwenyemaeneo mbalimbali nchini.Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ghala la mfanyabiashara huyo Kiwalani, Ilala, jijini Dar es Salaam, Mkaguzi wa TBS, Juma Nandule, alisema kukamatwa kwake kulitokana na taarifa kutoka wasamaria wema.Alisema Watanzania wengi wameshajua nguo hizo hazitakiwi kwenye soko letu, ndiyo maana baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa nguo hizo za ndani za mitumba walitoa taarifa TBS.Alisema, kwenye ukaguzi wa awali ulioanza Jumanne wiki iliyopita walifanikiwa kukamata mabelo matano kila moja likiwa na uzito wa kilo 100 na bado ukaguzi ulikuwa unaendelea. Alisema ukaguzi wa ghala la mfanyabiashara huyu bado unaendelea ili kuhakikisha nguo ambao hazitakiwi zinazuiwa na kuharibiwa. Alisema nguo hizo zinaondolewa kwenye soko kutokana na mamlaka ya shirika hilo chini ya sheria ya viwango namba 2 ya mwaka 2009.Alifafanua kuwa waagizaji wote wa mitumba walishaambiwa nguo za ndani za mitumba haziruhusiwi kwenye soko la Tanzania sasa. “Lakini bado wafanyabiashara wanakaidi na kuziingiza nchini kupitia njia za panya,” alisema na kusisitiza operesheni ya kuondoa nguo hizo za mitumba kwenye soko ni endelevu na awali walianza na wachuuzi wadogo kupitia misako inayoendelea kwa kushtukiza kwenye masoko.Alisema nguo hizo zina madhara kwa watumiaji hivyo alitoa mwito kwa Watanzania kuzikataa. Alisema nguo hizo zinachangia Watanzania kuendelea kuzitumia kutokana na bei kuwa ya chini.Akieleza sababu za kupigwa marufuku kwa nguo hizo za ndani za mitumba, Nandule alisema zimekuwa zikichangia magonjwa. Alipoulizwa hasara za waigizaji wa nguo za ndani za mitumba zilizopigwa marufuku, alisema ni kutozwa faini, kulipa gharama za ukaguzi wa mizigo, kulipa gharama za kuharibu shehena au kurudisha walikozitoa kwa gharama zao. | 3 |
MANCHESTER, England KIUNGO wa Manchester United, Nemanja Matic, amesisitiza kwamba wapo tayari kupambana na presha ya ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu. Kauli hiyo inatokana na mwanzo mzuri wa timu hiyo katika ligi hiyo. Ushindi wa mabao 4-0 mfululizo katika michezo miwili ya West Ham na Swansea, inakifanya kikosi cha kocha wa timu hiyo, Jose Mourinho, kuongoza msimamo wa ligi hiyo baada ya kujizolea pointi sita na mabao nane. Mourinho alikiri kwamba kikosi chake hakitapata ushindi kama huo kila siku hivyo wapo tayari kwa changamoto mpya itakayojitokeza. Lakini Matic, ambaye alijiunga hivi karibuni akitokea Chelsea, anaamini kwamba United inaweza kupambana na presha ya ubingwa na kulitwaa taji hilo msimu huu. “Unaweza kuwauliza wachezaji baada ya mchezo dhidi ya Swansea wanaweza kuwa na presha kutokana na mashabiki kutaka kuudhuria kila mchezo tutakaocheza kutokana na ubora wanaouona kwetu. “Kila siku United kuna kitu kipya, kuna presha lakini kwa sasa tupo tayari kupambana nazo,” alisema Matic. Matic alisema ana furaha kuwa United. “Wachezaji wote ni marafiki ndani ya vyumba vya kubadilishia nguo, jambo ambalo ni muhimu. “Msimu ni mrefu lakini kwa sasa tuna kikosi kizuri na mawasiliano mazuri pia, nafurahi kuwa miongoni mwao, huu ni mwanzo tu,” alisema Matic. Nyota huyo aliongeza kwamba ni jambo la muhimu kujiamini kabla ya kufikiri kufunga bao uwanjani kwani kufanya hivyo kunaweza kukusaidia kuwa makini katika kila mpira. “Kama unalinda vizuri unaposhambuliwa ni jambo zuri katika dakika 90 za mchezo, nina furaha kuwa miongoni mwa walinzi wanne wa United,” alisema Matic. | 4 |
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru), inatarajia kuwafikisha mahakamani askari sita wa Jeshi la Polisi na watendaji watatu wa vijiji wilayani Igunga, baada ya kuomba rushwa ya Sh milioni nane.Akizungumza na vyombo mballimbali vya habari ofisini kwake, Kaimu Kamanda wa Takukuru mkoani Tabora, Musa Chaulo alisema kwamba watu hao watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika . Alisema kwamba watendaji hao wa serikali, walimuomba rushwa mzee Ngaka Mataluma Fale (95) baada ya kumkamata, wakimtuhumu kuwa anajihusisha na tiba asilia bila kibali, kukutwa na mfupa unaodaiwa kuwa wa binadamu, kumiliki silaha za moto, kukutwa na mafuta ya simba, ngozi ya kenge na kukutwa na bangi.Chaulo alisema baada ya Fale kukosa kiasi hicho cha fedha, alitakiwa kuuza ng’ombe ili apate Sh milioni nane kwa ajili ya kutoa hongo kwa maofisa waliomkamata. Aliongeza kuwa Takukuru ilifanikiwa kukamata ng’ombe 11 wa Fale katika Mnada wa Igunga kwa wanunuzi, waliokuwa wakijiandaa kuwasafirisha kwenda Arusha.Alisema baada ya kuwakamata, imewarajesha kwa mhusika. Katika hatua nyingine, Kaimu Kamanda wa Takukuru mkoani Tabora Chaulo alisema katika robo iliyoishia Juni mwaka huu, Takukuru imefuatilia na kukagua miradi 40 ya maendeleo, yenye thamani ya Sh bilioni 9.285. Alisema kati ya miradi hiyo, saba inahusu sekta ya elimu, afya na ujenzi na ina thamani ya Sh bilioni 1.570. Miradi hiyo inafanyiwa uchunguzi. | 3 |
KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk Edwin Mhede amesema mamlaka za mapato kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zina tatizo la uadilifu.Amezitaka ziwe na uadilifu na kuongeza kiwango cha ukusanyaji mapato akisisitiza kuwa zinapaswa pia kutekeleza majukumu yake kwa uaminifu na weledi, ili kuziba mianya ya rushwa na ufisadi.Mhede ameyasema Dodoma hayo wakati wa kufungua mkutano wa 10 wa Mamlaka za Mapato ya Afrika Mashariki uliolenga kujadili na kuleta mbinu bora ya kukomesha tatizo la kukosa uadilifu.Mkutano huo ulilenga pia kujadili fursa na changamoto za mitandao ya kijamii katika kukuza uadilifu, kudhibiti athari za biashara haramu katika ukusanyaji mapato pamoja na kuzijua aina mpya za ufisadi, rushwa na kuzidhibiti."Kukosa uadilifu kumekuwa kukiharibu ukusanyaji ushuru na mapato mengine katika mkoa, kwenye picha pana tunashiriki masuala ya kawaida, ndiyo sababu tunahitaji kuangalia jinsi bora ya kuyashughulikia ili tuweze kuongeza mapato yetu,'' amesema.Kamishna wa Ukaguzi wa Ndani na Uzingatiaji wa Mamlaka ya Mapato ya Uganda (URA), Dk Begumisa Protazio aliyekuwa Mwenyekiti wa kikao hicho alisema bado kuna mambo mengi ya ufisadi katika kanda, hivyo maofisa wa mamlaka za mapato wanapaswa kuwa na nguvu."Wala rushwa ni wengi na wana nguvu, hivyo ikiwa unafikiria wewe ni dhaifu unaweza kubadilisha njia,'' alisema akiongeza kuwa viongozi wa mamlaka za mapato katika nchi sita za EAC kuwa makini na wenye weledi katika kudhibiti wahalifu hao.Alisema kwa kuwepo rushwa na kukosekana uadilifu, kunazifanya mamlaka za mapato kukosa wastani wa asilimia tano ya makadiriyo ya makusanyo.Alisisitiza haja ya kuja na njia bora kupambana kulingana na hali ilivyo kwa wakati huu.Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Mamlaka ya Mapato ya Afrika Mashariki, Esther Masibayi kutoka Kenya, amesema mkutano huo umelenga kuondoa utapeli katika vyombo vya ushuru ili kuongeza ukusanyaji wa mapato. | 3 |
Na AVELINE KITOMARY
“SITASAHAU siku ambayo nilijifungua mtoto wangu wa kwanza katika hospitali moja hapa jijini Dar es Salaam. Baada ya kujifungua mtoto yule, wahudumu walinitelekeza wakaniacha nisijue la kufanya. “Kwa sababu ya uchovu wa kujifungua, nilijikuta napitiwa na usingizi, ilipofika saa tisa usiku nilishtuka kutoka usingizini na kuona mtoto wangu akiwa amezidiwa na kubadilika rangi na kuwa wa kijani, niliogopa mno. “Nilivyoona hivyo nikatoka haraka huku nikikimbia kuelekea kule walikokuwa manesi, nilipofika niliwakuta wakiwa wamelala, nikawaamsha na kuwaambia wakamuone mtoto wangu amebadi lika rangi,” hii ni kauli ya Clara Mboya, mama aliyekumbwa na madhila wakati wa kujifungua mtoto wake wa kwanza. Licha ya kuwa mama wa watoto wa tatu sasa, uzazi wa mtoto wake wa kwan- za umemuachia kumbukumbu isiyofutia akilini mwake kutokana na changamoto alizokutana nazo wakati wa kujifungua. Clara anasimulia namna alivyoshikwa uchungu wa mtoto wake huyo wa kwanza na kufikishwa hospitalini (hakutaja jina la hospitali), lakini alivyofika na kupimwa akaambiwa njia ya uzazi bado haijafunguka. Jambo la kushangaza ni kwamba, licha ya kutoka mbali hadi kuifikia hospitali hiyo, alipofika hakupata ushirikiano wowote kutoka kwa muuguzi wa zamu, ambaye kwa makusudi hakutaka kumpa kitanda ili apumzike, badala yake alim- wambia arudi nyumbani. Anasema muuguzi huyo alimwambia kuwa njia yake haijafunguka hivyo anatakiwa kurudi nyumbani na arudishwe kesho yake. Anabainisha kuwa kwa kauli hiyo ya nesi walijikuta hawana namna yoyote zaidi ya kurudi nyumbani licha ya kwamba muda ulikuwa umekwenda ili kuwa ni majira ya saa kumi jioni. “Niliendelea kuumwa tumbo na mgongo, usiku mzima nilikosa usingizi huku nikijisikia vibaya, nilivumilia maumivu hayo hadi kulipokucha tukaanza safari ya kurudi tena hospitalini. “Tulivyofika nikamkuta yule yule nesi ambaye nilikutana naye jana yake akanirudisha nyumbani, nikamwambia
bado naumwa tangu jana, akanipima
tena akasema bado njia haijafunguka.
“Yule mama niliyeambatana naye
kwenda hospitalini akamwambia yule
nesi kwamba sasa hivi harudi nyumbani,
tunaomba kitanda apumzike na kama ni
mazoezi basi niendelee kuyafanya nikiwa
hapo,” anaeleza Clara.
Hata hivyo, anasema baadaye alipata kitanda huku akiendelea kufanya mazoezi hadi ilivyofika saa kumi ambapo uchungu ulianza kuchanganya na ku- pelekwa sehemu ya kujifungulia (leba). “Nilivyofika leba bado sikupatiwa hu- duma nzuri, nilikuwa nikiwaita manesi hawaji hasa ukizingatia kuwa walikuwa wawili tu, yaani ilikuwa unaita hadi unachoka hawaji mwishowe nikanyamaza. “Nilikuwa najisikia kujifungua lakini
ukimwita nesi haji, mwishowe niliishiwa
nguvu, kwa bahati nzuri akaja nesi
mmoja ambaye ni mwanamume, alikuwa
amemaliza zamu yake lakini sikusita
kumnweleza shida yangu.
“Nilimuita akaniuliza shida yangu
nikamwambia naumwa hadi nahisi
kuishiwa nguvu,” anasimulia Clara.
Anasema baada ya yule nesi kuonekana kumsikiliza, ilimlazimu kumuahidi fedha mara atakapomsaidia kujifungua salama. Anasema hata hivyo, nesi huyo
alikataa ofa hiyo akiahidi kumsaidia bila
malipo licha ya kwamba muda wake wa
kazi ulikuwa umekwisha.
“Namshukuru alinisaidia kwa kiasi
kikubwa hadi nikafanikiwa kujifungua
salama. Alikuwa akiniminya tumbo
kwa sababu nilishaishiwa nguvu kabisa,
sikuweza kufanya chochote bila msaada
wake.
“Mtoto aalipotoka akaniambia yupo
vizuri na alilia kama ambavyoinatakiwa,
kwa kifupi hakuwa na shida yoyote.
“Aliponikabidhi mtoto wangu
aliniambia nipumzike hadi kesho yake
asubuhi nitakapopata ruhusa ya kurudi
nyumbani,” anaelezea Clara.
Clara anasema changamoto hazi kuishia hapo kwani baada ya mtoto
kuzaliwa maziwa yalikuwa hayatoki
hali iliyosababisha mtoto alie mara kwa
mara.
“Mtoto alikuwa analia muda wote,
nawaita manesi na kuwaambia kuwa
mwanangu analia na huu ni uzazi wangu
wa kwanza, maziwa hayatoki sijui la
kufanya lakini hawakujali.
“Nilijaribu kuomba nisaidiwe maziwa
hata ya kopo ili nimpe mtoto anyamaze
lakini sikupata msaada wowote, badala
yake waliniambia kuwa anaweza kukaa
hadi kesho asubuhi bila kula chochote
na asipate shida.
“Kwa kuwa sikuwa nafahamu cho-
chote, niliwasikiliza na kuona kawaida,
nilijaribu kuminya maziwa kama yata-
toka lakini sikufanikiwa, nikaacha.
Anasema baada ya mtoto kulia kwa
muda muda mrefu, ndipo akabadilika,
aliwaita manesi na kuwaeleza ndipo
wakaanza kuangalia mafaili na kadi
yake.
“Baada ya hapo wakaniambia
niwasubiri watakuja, nilikaa kitandani
kuwasubiri huku natetemeka, mara
wakaja kumchukua.
“Asubuhi akaja nesi mwingine
tofauti na wale wa usiku. Aliniuliza
unajisikiaje nikamwambia nimeishiwa
nguvu natetemeka, akaniambia kwani
umetoka damu nyingi nikamwam-
bia sijui, akaniambia sawa nyanyuka
twende ukamwone mtoto wako.
“Nilipofika nilimkuta amewekewa dripu na wakaniambia kuwa wamemchoma sindano hivyo natakiwa kulipia. “Niliwaambia kwamba kwa wakati ule sikuwa na fedha, maana hata begi langu nilikuwa silioni kwahiyo hela italipwa kesho na baba yake atakapokuja, akasema Sawa,” anasimulia Clara. Anaeleza kuwa alivyorudi kitandani
akawa anatafakari sababu za mtoto
wake kuugua na kubadilika rangi.
“Ni kwanini wamenipa huduma
mbaya? Ukizingatia kuwa ilikuwa ni
hospitali binafsi, nililipia fedha nyingi
si kwamba nilikuwa natibiwa bure,
maswali haya yote yalikosa majibu,”
anahoji.
“Baadae nilitakiwa kwenda kum-
nyonyesha mwanangu, lakini nilipofika
sikumkuta yule mhudumu wa awali,
niliposimama mlangoni kumsubiri aka-
ja, akaniuliza wewe ni nani nikamtajia
jina langu na la mtoto wangu akasema
kanisubiri nitakuja kukuita.
“Nilimsubiri lakini hakuja, baadae
akaja nesi mwingine akaniuliza wewe
ndio fulani, nikamwambia ndio mimi,
akaniambia nieleze jinsi ulivyofika hadi
kujifungua… nikamweleza,” anasema.
Anasimulia kuwa baada ya
nesi huyo kupata maelezo yake
akamuuliza.”Nani wamekuja hadi sasa,
nikamwambia mume wangu amekuja
yuko nje, akaniambia nikamwite ili
twende ambako mtoto alikuwa ame-
pelekwa.
“Tulivyofika nikaambiwa mtoto
wangu amefariki, nililia kwa uchungu,
mume wangu alikuwa amekuja na
bahasha aliitupa pale pale akaondoka
zake,” anaeleza huku akifuta machozi.
WANAWAKE WANATAKA NINI?
Clara anasema suala la uzazi linahi-
taji huduma nzuri na wahudumu kuwa
karibu na wazazi.
Kwa wanawake wengine hili
limedhihirika baada ya Muungano
wa Utepe Mweupe na Uzazi Salama
Tanzania (White Ribbon), kufanya
kampeni katika maeneo mbalimbali
nchini.
Kampeni hizo zilizofanyika katika
mikoa ya Arusha, Dar es Salaam,
Dodoma, Kilimanjaro, Lindi, Mara, Mt-
wara, Mwanza, Shinyanga na Tabora,
ilihusisha wanawake na wasichana
110,000 kutoka mikoa hiyo.
Kwa mujibu wa Mratibu wa utepe
huo, Rosemary Mlaya, katika kampeni
hizo wanawake hao waliainisha map-
endekezo 10 waliyotaka yawepo katika
huduma za uzazi.
Anasema asilimia 8.99 ya wanawake
walipendekeza upatikanaji wa damu
salama inayotolewa bure, kuongezwa
kwa vifaa na vitendea kazi vya kujifun-
gulia.
“Asilimia 8.61 wanahitaji huduma za
uzazi zenye heshima na utu ambazo
pia ni rafiki na watoa huduma wenye
adabu. Asilimia 7.56 walihitaji huduma
zilizoboreshwa, ustawi na afya ya
uzazi.
“Asilimia 7.32 walihitaji kuongezwa
kwa vituo vya afya, vinavyofanya kazi
kwa ukamilifu na viwe karibu na kina
mama na wasichana huku asilimia 7.17
wakihitaji ushauri nasaha na ufahamu
kuhusu afya ya uzazi.
Mlaya anasema kitu kingine amba-
cho walikuwa wanakihitaji, asilimia
7.03 ya wanawake ni taarifa kuhusu
uchungu na kujifungua na uwapo wa
watoa huduma wakati wote.
“Wengine asilimia 5.41 walitaka kuongezwa watoa huduma wenye stadi na mazingira mazuri ya kazi kwa watoa huduma, wengine asilimia 4.41 walihitaji upatikanaji wa maji safi na vyoo safi na asilimia 4.18 walitaka uwapo wa vitanda, mashuka na magodoro,” anabanisha Mlay. Anasema Novemba mwaka jana, matokeo ya kampeni hiyo yaliwasilishwa bungeni ambapo jumla ya wabunge 60 wanaounda kikundi cha wabunge wabobezi wa masuala ya uzazi salama walishiriki, ikiwa ni pamoja na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. TAMKO LA SERIKALI
Katika kipindi cha miaka mitano,
serikali imekuwa ikiendelea na ujenzi
wa majengo maalum ya mama na mto-
to katika hospitali za rufaa ikiwamo
Mwananyamala.
Hatua hiyo inalenga kuboresha hu-
duma ili kupunguza vifo vitokanavyo
na uzazi. Mkurugenzi wa Huduma za
Kinga wa Wizara ya Afya, Maendeleo
ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Dk.
Leonard Subi, anasema utafiti mdogo
uliofanywa hivi karibuni unaonesha
vifo vitokanavyo na uzazi vimepungua
kutoka 1,744 mwaka 2018 hadi kufikia
1,657 kwa mwaka 2019.
Dk. Subi anasema sababu za kupun-
gua kwa vifo hivyo ni baada ya serikali
kuendelea kuboresha huduma za afya
ili kila mtu apate huduma bora hivyo,
mwananchi kupata huduma ni haki
yake.
“Katika kipindi cha miaka minne,
serikali imeweza kujenga hospitali 70
ambapo miaka zaidi ya 50 ya uhuru
kulikuwa na hospitali 77.
“Katika kila mkoa mpya tumejenga
hospitali na vituo vya afya 540 na
vingine kukarabatiwa.
“Tumeboresha Miundombinu ya vi- tuo vya afya 361 lengo letu ni kuwasikiliza wanawake wanachotaka hivyo, idadi ya kina mama wanaojifungulia vituo vya afya imeongezeka, mwanzo ilikuwa asilimia 63 lakini sasa wamefikia asilimia 79,” anabainisha Dk. Subi. Anasema upatikanaji wa dawa
umeongezeka ambapo sasa hivi dawa
muhimu zinapatikana kwa asilimia 94
huku chanjo zinapatikana kwa asilimia
98.
“Ongezeko hilo limetokana na
kuongezwa kwa bajeti ya dawa kutoka
Sh bilioni 30 hadi Sh bilioni 270.
Pia anasema serikali itachukulia kwa uzito vitu ambavyo wanawake wa navitaka ili waweze kufurahia huduma za uzazi ikiwamo mazingira bora. “Hivyo, vitu ambavyo wanawake
wanataka tutavichukua na kuvifanyia
kazi, tunataka wanawake wafurahie hu-
duma za uzazi kwa sababu ni sehemu
muhimu zaidi ya mwanzo wa binada-
mu, tutafuatilia mambo yote ikiwamo
hilo la kuongeza wahudumu wa afya,”
anaeleza Dk. Subi.
Pia anasema kwa kushirikiana na Taasisi ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na taasisi zingine za serikali na zisizo za kiserikali wa natarajia kukamilisha utafiti wa vifo vitokanavyo na uzazi. | 0 |
KITENDAWILI cha mrithi wa Gadiel Michael ambaye anatajwa kutua Simba akitokea Yanga kimejibiwa kwa Yanga kumsainisha beki wa kushoto wa Malindi ya Zanzibar, Muharami Salum ‘Marcelo’.Marcelo alisaini mkataba wa miaka mitatu kuichezea Yanga juzi usiku ikiwa ni siku chache baada ya beki huyo mwenye umri wa miaka 24 kusaini mkataba wa kuichezea Singida United pia ya Ligi Kuu Tanzania Bara.“Suala la mbadala wa Gadiel limemalizika, Yanga imekubaliana na Singida United imchukue Marcelo na tayari usajili wake umeshafanyika jana (juzi) usiku. “Hakuna pengo, Marcelo ni kijana mdogo na ana uwezo mkubwa wa kufanya kazi, Yanga wajisikie wenye furaha,” alisema mtoa habari wetu.Usajili huo wa Marcelo inamaanisha Yanga sasa imeachana rasmi na Gadiel, ambaye awali ilionekana kana kwamba anaisumbua klabu hiyo katika usajili.Mwenyekiti wa Yanga, Dk. Mshindo Msolla alipoulizwa jana kuhusu usajili wa beki huyo alisema Kamati ya Usajili ndiyo yenye jukumu la kuzungumzia.Hata hivyo alikiri klabu hiyo kutafuta mbadala wa Gadiel na kwamba beki huyo ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa na nafasi kubwa ya kusajiliwa Yanga.“Ni kweli kulikuwa na mazungumzo ya kumsajili Marcelo, sijapata taarifa mpya lakini naamini wakati wowote jambo lake litamalizika au limeshamalizika,” alisema Dk. Msolla.Yanga ilishindwa kumsainisha Gadiel Michael ambaye mkataba wake wa miaka miwili ulimalizika hivi karibuni, ikidaiwa beki huyo aliyetua Yanga akitokea Azam, alikuwa hatua za mwisho za kujiunga na Simba.Wachezaji waliosajiliwa Yanga hadi sasa ni kipa wa timu ya taifa ya Kenya, Farouk Shikalo, ambapo wachezaji wengine wa kigeni ni Issa Bigirimana, Patrick Sibomana, Sadney Urikhob, Maybin Kalengo, Juma Balinya, Lamine Moro na Suleyman Mustapha.Wachezaji wazawa waliosajiliwa kabla ya Marcelo ni Ally Mtoni ‘Sonso’, Ally Ally, Mapinduzi Balama na Abdulaziz Makame. | 4 |
TOKYO, Japan WAZIRI Mkuu wa nchi
hii, Shinzo Abe amesema kwamba mkataba
wa amani kati ya Serikali ya hapa na ya Urusi utaleta matokeo mazuri juu ya usalama katika Ukanda wa Asia na Pacific na pia utakuwa na manufaa kwa
Marekani ambao walisaini makubaliano ya
usalama na Tokyo. Waziri Mkuu huyo Abe
alitoa kauli hiyo jana mjini hapa katika mahojiano na Kitu Cha Televisheni cha NHK TV wakati akibu swali kuhusu mtazamo wake
endapo mkataba huo utasainiwa. Akijibu swali hilo,
Waziri Mkuu Abe alisema kwamba mkataba wa Usalama wa Marekani na nchi hii ni
msingi wa dhamana za usalama kwa taifa hili. “Mkataba wa
Usalama wa Japan na Marekani ni msingi
wa dhamana za usalama wa taifa la Japan,” alisema Waziri Mkuu Abe. “Na hatimaye
utakaposainiwa mkataba wa amani kati ya
Japan na Urusi utakuwa na matokeo mazuri
juu ya utulivu wa kikanda .. Nadhani hii itakuwa faida pia kwa
Marekani,”aliongeza waziri mkuu huyo. Alisema kwamba kiuhalisia
Urusi inashikilia visiwa vinne kikiwamo cha Kuril Kusini ambacho ili umuliki ake uweze
kurejeshwa kwa Japan yanatakiwa kufikiwa makubaliano kupitia mkataba huo. “Kuna mambo ambayo
tumeyapendekeza ili kutatua tatizo hilo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa
nchi hizi mbili,”alisema Waziri Mkuu Abe. Waziri Mkuu huyo alifafanua kuwa pia mawaziri
wa Mambo ya Nje wa mataifa haya mawili, Taro Kono wa Japan na Sergey Lavrovwa Urusi watakutana mjini Moscow Januari 14 mwaka huu kwa ajili ya kuzungumzia suala
hilo. | 2 |
NAIBU Waziri wa Madini, Dotto Biteko amemwagiza Ofi sa Madini Mkazi wa Kanda ya Mirerani kuhakikisha anaufungua Mgodi wa Gem and Rock Venture na kuanza kufanya kazi mara moja, lakini kwa kufuata masharti ya leseni, kanuni, mipaka na sheria za uchimbaji na sio vinginevyo.Biteko alitoa agizo hilo juzi katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara baada ya kupokea taarifa za pande zote mbili juu ya mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka miwili baada ya Kampuni ya Gem and Rock Venture iliyopo Kitalu B kutoboa Mgodi wa Kitalu C unaomilikiwa na Kampuni ya TanzaniteOne. Alisema serikali iko kwa ajili ya kusimamia sheria na haki kwa wachimbaji wote, wawe wakubwa au wachimbaji wadogo, kwa lengo la kutaka kila mmiliki wa mgodi kufuata sheria ya leseni ya uchimbaji aliyopewa na wizara.Alimwagiza Ofisa Madini Kanda ya Mirerani, Daudi Ntalima kabla ya kuwaruhusu Gem and Rock kuhakikisha anakagua mgodi huo kwanza ili ajiridhishe ikiwamo kuangalia usalama wake, wamiliki wanafuata sheria ya leseni yao ya uchimbaji, kanuni na mipaka ya mgodi na wakifuata masharti hayo, wanapaswa kuruhusiwa kuanza kazi. Akizungumzia malipo kutoka kwa wachimbaji wadogo ambayo walikuwa wakilipwa TanzaniteOne bila mbia Shirika la Madini la Taifa (Stamico) kufahamu, aliwataka Stamico kuamka na kufuatilia kila kitu kinachofanywa na mbia mwenza.Aliwataka Stamico kukaa kibiashara zaidi kwa kufuatilia kila kitu ikiwamo kuangalia mikataba inayoingiwa na mbia mwenza na malipo mengine ambayo yanaweza kuwa nje ya sheria ya leseni ya madini. “Nimekuagiza RMO (Ofisa Madini Mkoa) kuhakikisha Gem and Rock Venture wanafunguliwa mgodi, lakini kabla ya kuwafungulia hakikisha unakagua mgodi wao kama umefuata sheria za madini, mipaka na kanuni,” alisema.Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila, alisema ofisi yake itahakikisha inaangalia mipaka ya Mgodi wa Kitalu C na mpaka wa Kitalu B kama yote iko kisheria na nani anastahili kuifuata, kwa lengo la kuepuka migogoro isiyokuwa na tija kwa wachimbaji wakubwa na wachimbaji wadogo. Alisema serikali haiko ili kumnyanyasa mtu yeyote, bali iko kuhakikisha kila mchimbaji kote nchini anapaswa kufuata sheria ya leseni aliyopewa, mipaka na kanuni na ikikiukwa serikali haitakuacha salama.Mkurugenzi Mwenza wa TanzaniteOne, Faisal Juma alisema kampuni hiyo inafuata sheria za leseni waliyopewa na kamwe hawawezi kufanya kazi nje ya masharti ya leseni. Juma alisema mara nyingi wachimbaji wadogo wamekuwa wakivamia mgodi wa TanzaniteOne, wao hawajawahi kuvamia migodi ya wachimbaji wadogo kama inavyoelezwa kwani kampuni hufanya kazi kwa kufuata mpango wa madini ambao unatoa mwelekeo wa uchimbaji salama wenye kufuata sheria. Alisema wakati wanapewa uwekezaji katika mgodi huo, waliona mipaka na majira ya nukta (Cordnets) katika mikataba hivyo wao wanafanya kazi kwa kufuata mipaka hiyo na sio vinginevyo.Akizungumzia suala la kufanya kazi bila kushirikisha Stamico, alisema suala hilo sio sawa kwani wanafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa kupitia MEU (Kitengo cha Ufuatilia na Tathamini), na hakuna kitu kinafanywa bila wao kujua kwani hukaa kila siku asubuhi katika vikao vya menejimenti kufahamu utendaji kazi ndani na nje ya mgodi. Mgogoro kati ya Gem and Rock Venture na TanzaniteOne uliodumu kwa miaka miwili, ulitokana na Gem and Rock kuingia kinyemela na kufanya kazi katika mgodi wa TanzaniteOne mita zaidi 640 kinyume na leseni yao. Kutokana na hali hiyo, Ofisa Madini Mkazi alichukua hatua ya kuufungia mgodi huo na kuamriwa kurudi nyuma kama kanuni za mitobozano zinavyosema. | 3 |
NA VERONICA ROMWALD– DAR ES SALAAM SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA), wameipa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto magari 58. Who imetoa msaada wa magari 50 ya kubebea wagonjwa (Ambulance) na UNFPA imetoa magari manane ambayo yatatumika kuratibu shughuli za afya ya mama na mtoto. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya makabidhiano ya magari hayo, Waziri Ummy Mwalimu, alisema yatagawiwa katika mikoa sita iliyopo Kanda ya Ziwa. “Tafiti zilizofanywa mwaka 2010 na tathmini iliyofanywa mwaka 2015 wakati wa kuandaa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN), mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwamo Kigoma ilionekana kuwa na viashiria hafifu vya afya ya mama na mtoto,” alisema. Akitolea mfano alisema mikoa hiyo ilionekana kuwa na utumiaji mdogo wa huduma ya uzazi wa mpango, wanawake wachache ndio waliojifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya na kuna idadi kubwa ya vifo. “Wanawake wengi wanafariki dunia kwa uzazi nchini, hii ni changamoto kubwa kwetu, tumepambana kwa miaka 20 tumefanikiwa kuvipunguza kutoka vifo 580 hadi 432 kwa kila vizazi hai 100,000. “Nia yetu ifikapo 2020 tuweze kupunguza tena idadi hiyo kutoka 432 hadi 292 sawa na asilimia 30 pamoja na vifo vya watoto wachanga kuvipunguza kutoka 54 ya sasa hadi 40 kwa kila vizazi hai 1,000,” alisema na kuongeza: “Hivyo magari haya yatapelekwa katika mkoa wa Mwanza, Geita, Kigoma, Simiyu, Kagera na Mara. Aliwataka waganga wakuu wa mikoa ambao watakabidhiwa magari hayo kuyakatia bima ya ajali ili yaendelee kudumu kutoa huduma kwa wananchi. Mwakilishi Mkazi wa UNFPA-Tanzania, Dk. Hashina Begum, alisema magari hayo manane waliyoyatoa yana thamani ya Sh milioni 387. “Tuna imani kwamba yatakuwa msaada mkubwa kwa Serikali katika kusimamia shughuli zote za uratibu wa afya ya mama na mtoto na hivyo kufikia lengo la kupunguza idadi ya vifo iliyotajwa,” alisema. Naye Mkurugenzi Mkazi wa WHO, Dk. Grace Saguti, alisema ambulance hizo zilizotolewa zitakuwa na huduma zote muhimu. “Tumetanguliza hizi 50 zenye thamani ya Sh bilioni 5.9, lengo letu ni kuipatia wizara ya afya jumla ya ambulance 67,” alisema. | 3 |
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amezindua mpango mkakati wa taifa wa miaka minne wa masikio na usikivu na kuahidi kuwa serikali itahakikisha huduma hizo zinatolewa hadi ngazi ya chini.Akizungumza wakati wa kuzindua mkakati huo uliokwenda sambamba na kambi ya wazi ya kutolewa huduma kwa jamii ya wenye matatizo ya masikio na usikivu jijini hapa, Ummy alisema tatizo hilo lipo katika jamii ya Watanzania. “Pamoja na kuwa hakuna takwimu rasmi za kitaifa, lakini takwimu ndogondogo zinaonesha asilimia tatu ya watoto walio shuleni wana matatizo ya masikio na usikivu wa hatua mbalimbali, lakini pia liko kwa watumishi wa migodini na wale wanaofanya kazi kwenye viwanda,” alisema.Alisema kutokana na tatizo hilo, serikali iliamua kuanza kutoa matibabu ya kibingwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo katika kipindi cha miaka miwili watoto 26 wametibiwa kwa gharama ya Sh milioni 35 huku mamia wakiwa kwenye foleni.“Kabla ya kuanza kutoa tiba hiyo hapa nchini, serikali ilikuwa ikipeleka wastani wa watoto 13 kila mwaka ambapo kila mmoja alikuwa akigharimu kati ya Sh milioni 80 hadi 100, lakini sasa tumeweza kuokoa fedha kwa kutoa huduma hi,” alieleza. Alisema kutokana na uhitaji wa huduma hiyo ni mkakati wa serikali kuhakikisha huduma hizo zinatolewa katika ngazi za chini na hospitali zingine za mikoa na wilaya na kuutumia mkakati huo kama mwongozo.Ummy alisema pia serikali imeweza kuongeza wataalamu na madakatari wa pua, koo na masikio kutoka wataalamu 11 waliokuwapo mwaka 2009 hadi kufikia kuwa na wataalamu 46 mwaka 2018, ingawa idadi hiyo bado ni ndogo. Aidha, Ummy alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa jamii kutunza masikio, kuwa na matumizi sahihi ya dawa, kuwa makini na vijiti vya kusafishia masikio ambavyo ni moja ya visababishi vya matatizo ya masikio na usikivu.“Pia tujihadhari na matumizi ya spika za masikioni hasa kwa vijana, unaweza kuona unakwenda na wakati lakini kumbe tunatengeneza kizazi chenye matatizo ya masikio na usikivu,” alisema.Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka wizarani, Dk Grace Magembe alisema watatumia mkakati huo katika kupanua utoaji wa huduma za pua, koo na masikio. Mmoja wa waanzilishi wa taasisi ya Starkey, Bill Austin alisema matatizo waliyobaini katika kambi za wazi ni ya masikio na usikivu ambayo yanaweza kutibika endapo tu mgonjwa atapatiwa tiba mapema.Taasisi ya Starkey Foundation for Ear and Hearing care, kabla ya kufanya Dodoma ilifanya kambi kama hiyo jijini mwanza ambapo watu zaidi ya 2,000 walipewa vifaa vya kusaidia usikivu. | 3 |
Onesho hilo lililoanza saa sita mchana na kumalizika saa nne usiku lilihusisha pia wasanii wengine wa hapa nchini kama akina Feza Kessy na Ali Kiba.Kundi la Sauti Sol la Kenya, ambapo tangu mwanzo hadi wanamaliza mashabiki walishindwa kujizuia na kushangilia wakati wote.Katika onesho hilo ambalo lilikuwa ni la muziki wa Live, kundi hilo lilifanikiwa kuimba na kuwavutia mashabiki wao ambapo waliwachezesha muziki huku wakiimba nao nyimbo zao mbalimbali.Mbali na kuimba nyimbo zao pia walichanganya na nyimbo za Kikongo na walicheza kama Wakongo pia walikuwa wakicheza kwa staili moja huku wakiwa wamevalia sare ya nguo nyeupe.Mbali na wao kucheza lakini pia waliwaalika jukwaani watu na kuimba nao pamoja ambapo kuna wakati waliwapandisha jukwaani mashabiki wao na kuwachezesha nyimbo zao.Wasanii hao walipoanza kuimba wimbo wao unaotamba kwa sasa wa Usitoe Mimba Yangu na walitaja majina mbalimbali makubwa ya watu wenye sifa katika jamii na kuna muda waliwataja Mwalimu Nyerere pamoja na Kikwete na hivyo mashabiki walijikuta wakiwashabikia kwa shangwe.Mwisho walimalizia na wimbo wao wa Sura Yako Nzuri na hadi wanatoka jukwaani watu walikuwa wanaonekana bado wanawahitaji kuendelea kuimba. Walipomaliza akapanda jukwaani Ali Kiba aliimba nyimbo zake kadhaa na yeye alikuwa akiimba live na kisha wakaja kupanda jukwaani Mafikizolo.Kundi hili lilianza kwa shangwe pia ambapo walianza kwa kucheza shoo yao kwanza na kisha wakaanza kuimba nyimbo zao. Kundi hilo lilifanikiwa nalo kuzikonga nyoyo za mashabiki wao na hasa kwa kutokana na walivyokuwa wakicheza na kurukaruka jukwaani hapo. | 4 |
SERIKALI imekabidhi vipima ulevi kwa ajili ya wasimamizi na madereva wa treni za abiria na mizigo ambavyo vitasaidia kubaini kiwango cha ulevi.Vifaa hivyo vimetolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kwa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) na Shirika la Reli Tanzania (TRC).Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe amesema wametoa vifaa hivyo kuhakikisha usalama unakuwapo na matukio ya ajali yanapungua kutokana na ushughulikia ulevi unaoathiri miundombinu na maisha ya watu.Ngewe amesema vifaa vitano vimekabidhiwa kwa Tazara na 11 kwa TRC. Kaimu Mkurugenzi wa Reli katika Sumatra, Lameck Kamando alisema vifaa hivyo kila kimoja kina uwezo wa kuhifadhi matukio 65,000 na kina uwezo wa kutoa taarifa za mahali tukio liliporekodiwa (GPS).Vina uwezo wa kuhamisha taarifa kwenda kwenye kompyuta, na kuchaji kwenye gari, umeme wa nyumbani. Vina kifaa maalumu cha kuhifadhi chaji, uwezo wa kufanya kipimo kila baada ya sekunde 30 na inafanya kazi kwenye mazingira ya joto na baridi.Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema vitasaidia kubaini kiwango cha ulevi kwa wafanyakazi wa treni kabla ya kuanza safari, wawapo safarini na wanapomaliza safari ili kudhibiti ipasavyo matukio hatarishi na ajali zinazoweza kujitokeza.Kamwelwe alisema ajali zinazosababishwa na makosa ya kibinadamu ni nyingi.Alisema asilimia 65 ya ajali zinazotokea kwenye reli zinachangiwa na makosa ya kibinadamu ukiwamo ulevi. Pia kwa upande wa barabara asilimia 80 huchangiwa na makosa hayo.“Kwa kuwa serikali imewekeza na inaendelea kuwekeza katika usafiri wa reli, juhudi hizi haziwezi kuzaa matunda endapo waendeshaji na watoa huduma wa vyombo husika hawatakuwa makini kulinda usalama wa abiria, mizigo, vyombo na miundombinu hiyo,” alisema Kamwelwe.Alisema makabidhiano ya vifaa hivyo ni ishara ya namna serikali inavyozingatia kwa vitendo usalama katika reli.Alisema serikali inategemea baada ya kuanza kutumika vifaa hivyo, vihatarishi au matukio ya ajali zinazotokana na makosa ya kibinadamu zitapungua.“Iwapo vifaa hivi vitatumika ipasavyo tutajihakikishia usalama wa abiria, mizigo na wafanyakazi wenyewe na kuweza kufikia azma ya Tanzania ya viwanda kwa kupunguza ajali na kuongeza tija katika huduma za reli,” alisema.Waziri alitoa mfano wa ajali za hivi karibuni ni pamoja na tukio la Agosti 29 ambalo treni za mizigo kugongana uso kwa uso kati ya stesheni za Itulu na Tabora. Lingine ni la Agosti 13 mwaka huu la treni ya abiria kushindwa kusimama kwenye stesheni ya Malongwe na baadaye dereva kulazimika kurudi nyuma.“Ni dalili tosha za kukosekana kwa umakini na viashiria hatarishi katika uongozaji na uendeshaji wa treni,” alisema na kusisitiza kuwa vifaa hivyo vitafupisha uchunguzi wa ajali iwapo itatokea kwani suala la ulevi halitakuwa na nafasi.Aliagiza Tazara na TRC kuwachukulia hatua za kisheria watakaobainika kufika kazini wakiwa wamelewa au kutumia kilevi wawapo kazini.“Tumezoea kusikia kuwa hatua hazichukuliwi kwa kusubiri uchunguzi, suala la kumbaini mfanyakazi aliyetumia kilevi halina uchunguzi zaidi ya matokeo mara baada ya kupima ulevi,” alisema.Alikitaka Chama cha Wafanyakazi wa Reli (TRAWU) kuendelea kuelimisha wafanyakazi juu ya madhara ya ulevi na matumizi ya kilevi kazini.“Trawu iwe ya kwanza kuwakemea na ikiwezekana iwe ya kwanza kuripoti matukio ya aina hiyo kwenye vyombo husika. Mara nyingi mmekuwa mkionekana kuwatetea wafanyakazi wanapochukuliwa hatua na kudai kwamba wameonewa, lakini wanapofanya makosa hamuwaonyi, badilikeni,” alisema waziri.Meneja Mkuu wa Tazara Tanzania, Fuad Abdallah alisema maagizo yote wameyapokea na watayatekeleza.Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa alisema watatekeleza na kutoa mrejesho lengo likiwa ni kuhakikisha usafiri wa reli unakuwa wa uhakika na salama wakati wote. | 3 |
Na ALLY BADI
-LINDI
MKE wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Salma Kikwete, amemshukuru Rais Dk. John Magufuli kwa kumwona na kumteua kuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Salma ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM akitokea Wilaya ya Lindi Mjini, alitoa shukrani hizo wakati alipopewa nafasi ya kutoa salamu kwa wakazi wa Kata ya Ngapa waliohudhuria ziara ya Rais Magufuli ya kukagua mradi wa maji wa eneo hilo.
Salma ambaye yupo mkoani Lindi, alijitokeza jana katika ziara ya Rais Dk. Magufuli mkoani humo ambapo mbali na kutoa shukrani hizo alisema tatizo la maji katika Manispaa ya Lindi limekuwa kero ambayo inanyima utulivu kwa watendaji na viongozi wa wilaya na mkoa huo kwa ujumla.
Katika hilo alisema kwa nafasi aliyopewa atahakikisha anawawakilisha vyema wananchi wa Lindi na atashirikiana na wabunge wa mkoa huo kutatua kero ya maji.
Uteuzi huo wa Salma umekuja ukiwa umepita zaidi ya mwaka mmoja tangu jina lake litajwe na kuhusishwa katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini.
Tetesi za Salma kuhusishwa na kinyang’anyiro hicho zilififia baada ya yeye mwenyewe kushindwa kujitokeza katika kinyang’anyiro hicho wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka 2015.
Kwa upande wake Rais Magufuli katika ziara hiyo ambayo alikuwa ameambatana na Mama Salma lakini pia viongozi kadhaa wa kiserikali, kisiasa na mkoa akihutubia baadaye katika Uwanja wa Ilulu alimsifia akisema:
“Nimewaongezea Salma ni mchapakazi, anakipenda chama naamini kupitia yeye nitajua changamoto, hata mzuri ni mzuri jamani au naongopa? Naongea hayo Kikwete hayupo angerusha ngumi lakini naamini hatasikia,” alitania Rais Magufuli huku akiangua kicheko na kupokewa na shangilio kutoka kwa watu waliokusanyika kumsikiliza na wengine walisikika wakipiga vigelegele.
Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Lindi, Hamida Abdalah, alimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua Salma kuwa mbunge na kuongeza kuwa kitendo hicho cha kuwaongezea wawakilishi wananchi kitaleta ufanisi na maendeleo kwa mkoa huo.
Amina Chapunga mkazi wa Ngapa, alisema kuteuliwa kwa Mama Kikwete kuwa mbunge kumeonyesha jinsi alivyokuwa karibu na jamii na kuwatumikia wananchi wakati alipokuwa mke wa rais.
Fatuma Khatibu alisema kitendo hicho kimeleta gumzo na mshangao mkubwa kwa wakazi wa Lindi.
“Unajua tunachoshangaa mke wa rais tena kuwa mbunge kwani ubunge na mke wa rais mkubwa nani? Hivi tumeshindwa kufaidika akiwa mke wa rais tutafaidika akiwa mbunge?” Alishangaa Fatuma Khatibu.
Kumekuwa na mitazamo mbalimbali baada ya Jumatano wiki hii Rais Magufuli kumteua Salma kuwa mbunge.
Wakati wengine wakisifia na kutaka watu wasiunganishe uteuzi huo na Rais Mstaafu Kikwete, wapo ambao wamekuwa na mtazamo tofauti wakihusisha na uamuzi huo na mfumo wa utawala wa kulindana na kuendelezana. | 3 |
Aveline Kitomary -Dar es salaam MWENYEKITI
wa Chama cha Lupus Awareness and Support Foundation (LASF), Hajrrath Mohamed, ameitaka
jamii ibadilishe mtazamo hasi kuhusu ugonjwa wa Lupus ambao unahusishwa na Ukimwi
huku akikemea matukio ya unyanyapaa kwa wanaougua. Akizungumza
na MTANZANIA Dar es Salaam juzi, Hajrrath alisema hali ya ugonjwa wa Lupus kuhusishwa
na ushirikina pia inawapa wakati mgumu wagonjwa hao. “Lupus
ni ugonjwa wa kurithi, unatokea pale kinga za mwili zinapoacha kazi ya kulinda
na badala yake kushambulia mwili. “Lakini
watu wengi hawana uelewa kuhusu ugonjwa huo, hivyo wagonjwa wamekuwa wakipata
shida kutokana na jamii inayowazunguka kuwa na mitazamo hasi. “Wapo
wanaohusisha ugonjwa huo na Ukimwi na wengine wanaamini ugonjwa huo ni kulogwa
kitu ambacho si kweli, hali hiyo imefanya wagonjwa wasiweze kujiamini hata
katika utendaji wa kazi zao, pia tunanyanyapaliwa sehemu za shule hata za
kazi,” alisema Hajrrath. Alieleza
kuwa changamoto hizo zinazojitokeza zinawafanya wagonjwa wengi wa Lupus
kushindwa kujitokeza hadharani na kubakia kujificha. “Wakati
naanza kupata ugonjwa wa Lupus nilikuwa naogopa kuonana na watu, hata kutoka
nje ya nyumba naogopa kwa sababu watu wananiangalia sana, wengine wananisema
vibaya, hivyo nilikuwa nakaa tu chumbani, hata wageni wakija sitoki chumbani. “Nawatia
moyo wagonjwa wa Lupus wasijifiche, wajitokeze ili chama kiweze kuwajua na
kuungana pamoja kama chama, hivyo kila mmoja ajikubali kwa jinsi alivyo,” alishauri. Hajrrath
ambaye ni mwanzilishi wa chama hicho, alisema malengo hasa ni kujua idadi ya
wagonjwa, kukabiliana na changamoto za wagonjwa wa Lupus na pia kutoa elimu kwa
jamii. “Mpaka
sasa tokea mwaka jana kwa Mkoa wa Dar es Salaam wagonjwa waliojitokeza ni 12,
lakini wengine bado hawajiamini. Tukiwa wengi pia na sisi Serikali itatuangalia,
tutapata dawa,” alisema. Hajrrath
aliiomba Serikali kuuangalia ugonjwa huo kwa jicho la tatu kwani bado wagonjwa hupata
changamoto nyingi ikiwamo za dawa na madaktari. | 0 |
Kulwa Mzee -Dar es
Salaam MAHAKAMA
ya Rufaa imetupilia mbali maombi ya marejeo yaliyowasilishwa na aliyekuwa Mkuu
wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, SP Christopher Bageni na kubariki adhabu ya
kunyongwa hadi kufa iliyotolewa na mahakama hiyo kwa sababu haikukosea kufikia
uamuzi huo. Hukumu hiyo imetolewa jana na kusomwa na Naibu Msajili
Mwandamizi, Elizabeth Mkwizu, baada ya jopo la majaji watatu, Stellah Mugasha, Ferdinand
Wambali na Rehema Kerefu kusikiliza hoja za pande mbili zilizowasilishwa na
kuona kwamba mrufani kashindwa kuishawishi mahakama. Bageni
alipewa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kuwaua kwa makusudi
wafanyabiashara wanne wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva teksi katika
Msitu wa Pande, Dar es Salaam. Akisoma
uamuzi wa jopo hilo, Naibu Msajili Mwandamizi, Elizabeth alisema hakuna ubishi
kwamba Bageni alikuwa ni ofisa wa polisi wa cheo cha juu na kwamba katika Msitu
wa Pande alikuwepo. Alisema
hoja ya mrufani kwamba wakati wa kutiwa hatiani mahakama ilizingatia hoja mpya
haina mashiko, kwa sababu hakuna kitu kipya, Mahakama ya Rufaa ni wajibu wake
kuangalia kilichotokea katika ushahidi na kwa kufanya hivyo si kuleta mambo mapya. Naibu Msajili Mwandamizi, Elizabeth alisema mahakama ilipomtia hatiani Bageni ilizingatia
ushahidi wa mshtakiwa mwenzake, Koplo Rajabu Bakari na ushahidi huo uliungwa
mkono na mwenendo wake baada ya tukio la mauaji. “Koplo
Rajabu alisema Bageni alikuwepo Msitu wa Pande muda wote na ndiye aliyeamuru wafanyabiashara
hao wapelekwe huko. “Wakiwa
msituni, Rajabu alibakia katika gari na redio call akasikia milio ya risasi,
aliifuata akakuta mtu wa mwisho anamaliziwa kupigwa risasi na Koplo Saad. “Anasema
hakusikia katika redio kwamba Bageni aliamuru wapigwe risasi, lakini aliamuru
wapelekwe msituni, lakini si aliyeua. “Ushahidi
wa Koplo Rajabu uliungwa mkono na mwenendo wa Bageni baada ya tukio kwani
alidanganya kwamba kulikuwa na mashambulizi ya risasi kati ya polisi na
majambazi wakati baadhi ya mashahidi walisema hapakuwa na mashambulizi hayo. “Bageni aliamuru askari wawili waende baharini
kufyatua risasi tisa na kisha alichukua maganda na kudai yalipatikana Sinza
katika mashambulizi. “Mtu yeyote anayedai mahakama ilikosea kufikia
uamuzi alitakiwa yeye athibitishe madai hayo, kwa mazingira hayo mrufani
kashindwa kuishawishi mahakama kuona kwamba ilikosea kufikia maamuzi hayo,
hakuna namna nyingine zaidi ya kutupilia mbali maombi ya mrufani,” alimaliza
kusoma Naibu Msajili. Mrufani
aliyewakilishwa na wakili wake Gaudioz Ishengoma, aliwasilisha maombi ya marejeo
dhidi ya hukumu iliyotolewa Septemba 13
na kusomwa Septemba 16 mwaka 2016 na aliyekuwa Msajili wa Mahakama hiyo, John
Kahyoza. Mleta
maombi alitiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu hiyo na jopo la majaji watatu, Jaji
Benard Luanda, Sauda Mjasiri na Senistocles Kaijage. Akiwasilisha
sababu mbili za kuomba marejeo, Ishengoma alidai mteja alinyimwa haki ya
kusikilizwa wakati wa kutathmini ushahidi ulioko kwenye kumbukumbu za mahakama
kwa kuegemea tu kwenye ushahidi wa upande wa mashtaka. Alidai
katika kuchanganua ushahidi ambao uamuzi wa mahakama uliegemea, mahakama
ilishughulika na ushahidi wa msingi (Exam in Chief) wa upande wa mashtaka na
iliangalia kwa juu juu tu ushahidi wa utetezi, hususan wa Bageni au
haikuutazama kabisa. Ishengoma
alidai mahakama ilimtia hatiani mrufani kwa hoja ambazo hazikujadiliwa wakati
wa usikilizwaji wa rufaa iliyokatwa na Jamhuri, wakipinga Mahakama Kuu
kuwaachia huru washtakiwa. “Mahakama Kuu ilisema kwamba washtakiwa wote
walikuwepo msituni, lakini mahakama haiwezi kumtia hatiani mtu aliyesaidia
mauaji na kumwacha aliyeua, hivyo inawaachia huru,” alidai. Alidai
Mahakama Kuu ilisema kosa la kuua na kosa la kusaidia kuua ni makosa mawili
tofauti, si sahihi kwa mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji kutiwa hatiani kwa kosa jingine
ambalo tangu mwanzo mshtakiwa alitakiwa kulijua ili aweze kujitetea. Ilisema makosa
hayo si makosa yanayofanana, hivyo mahakama hiyo ilitofautiana na hoja za upande
wa Jamhuri kwamba washtakiwa watiwe hatiani kwa kosa la kusaidia kuua baada ya
kushindwa kutiwa hatiani kwa mauaji. “Jamhuri katika sababu za kukata rufaa
walitaka washtakiwa wote watiwe hatiani kwa sababu walionekana wote walikuwepo
msituni Pande. “Mahakama
badala ya kujikita katika eneo hilo, yenyewe ilijiuliza maswali kwamba walienda
Pande kufanya nini, walipelekwa na nani, hoja ambazo hazikuwepo katika sehemu
ya mabishano, mrufani alijikita kujibu sababu za rufaa na si maswali
yaliyoibuliwa na mahakama,” alidai. Alidai
katika utetezi wake, Bageni alisema hakwenda msituni, lakini mahakama
ilipochambua ushahidi iliangalia ushahidi wa upande wa Jamhuri na kuacha
utetezi wa mshtakiwa na haikusema chochote kuhusu utetezi huo. Akizungumzia
sababu ya pili ya kuomba marejeo, alisema kulikuwa na dosari ya wazi katika
kumbukumbu za mahakama. Wakili wa
Serikali Mwandamizi, Ladislaus Komanya, akijibu hoja za mleta maombi, alidai
anapinga maombi yaliyowasilishwa na kwamba mleta maombi alisikilizwa sana. Bageni alikuwa
mshtakiwa wa pili na katika hukumu iliyotolewa na Jaji Salum Massati mwaka 2009
wote waliachiwa huru, lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hakuridhishwa na
uamuzi huo, hivyo alikata rufaa dhidi yao katika rufaa namba 358 ya mwaka 2013. Kabla ya
usikilizwaji wa rufaa hiyo, DPP aliwaondolea rufaa wajibu rufaa watano na
kubaki wajibu rufani wanne ambao waliachiwa huru pia Septemba 16 mwaka huu. Walioachiwa
huru ni aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO) Kamishna
Msaidizi wa Polisi Abdallah Zombe na Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Ahmed
Makelle na Rajabu Bakari baada ya mahakama kuona hakuna ushahidi wa wazi ama
mazingira kuwatia hatiani. Katika
kesi ya msingi, Bageni alidaiwa kuwaua kwa kukusudia wafanyabiashara Sabinus
Chigumbi, maarufu Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na
Juma Ndugu, aliyekuwa dereva wa teksi wa Manzese , Januari 14, mwaka 2006,
katika Msitu wa Pande Mbezi Luis akahukumiwa kunyongwa hadi kufa. | 3 |
Na TUNU NASSOR -DAR ES SALAAM MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi kavu na Majini (SUMATRA), imewataka wadau wa bandari nchini kuanza utumaji wa nyaraka kwa njia za kielektroniki ili kurahisisha uondoshaji wa mizigo. Akizungumza na wadau hao juzi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema baadhi ya wamiliki wa kampuni za meli wamekuwa hawatekelezi agizo hilo na hivyo kusababisha kuongeza gharama zisizo za lazima. Alisema kuanzia jana wamiliki hao wanatakiwa kutumia njia za kielektroniki katika kutuma nyaraka za mizigo. “Mnatakiwa kutumia njia za kielektroniki kutuma nyaraka kuanzia kesho(jana) ama sivyo nitawanyang’anya leseni za usajili,” alisema Ngewe. Ngewe aliwataka pia wamiliki wa bandari kavu(ICDs) kuacha tabia za ucheleweshaji wa makusudi wa uondoshaji wa mizigo bandarini kwa nia ya kujipatia fedha zaidi. “Mnatakiwa kusoma alama za nyakati ucheweji wa kwenda kutoa mizigo bandarini ili kuwaongezea gharama wateja muache mara moja kabla hatujawachukulia kali,” alisema Ngewe. Awali Katibu wa Chama cha Mawakala wa Forodha(TAFFA), Tony Swai alilalamikia nyaraka kutokutolewa kwa njia ya kielektroniki huku wakitakiwa kulipa fedha kiasi cha Dola za marekani 45 kwa kila nyaraka wanayoihitaji katika kutoa mzigo. “Upatikanaji wa nyaraka za mizigo unachukua kati ya siku mbili hadi nne huku ICDs nao wanakwenda kuutoa baada ya muda mrefu ili kutuongezea gharama mawakala hii inafanya wadau wengine kuikimbia bandari,” alisema Swai. | 3 |
Timu hiyo ilishindwa kucheza mechi zake dhidi ya Prisons na Mwadui ya Shinyanga za Ligi Kuu ya Tanzania Bara ili kuipisha timu hiyo kushiriki mechi za kimataifa za kujipima nguvu zilizoshirikisha timu nne kutoka Zambia, Zimbabwe na Tanzania.Katika michuano hiyo iliyoshirikisha pia timu za wenyeji, Zanaco FC na Zesco United pamoja na Chicken Inn ya Zimbabwe, Azam FC iliibuka bingwa. Azam FC itamenyana na Prisons Februari 24, mwaka huu Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya kabla ya kumenyana na Stand United Machi 16, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.Lakini timu zote zitaendelea na ratiba iliyopo ya Ligi Kuu, Azam FC ikimenyana na wenyeji Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga Jumapili, wakati Stand United wataikaribisha Simba Jumamosi mjini Shinyanga na Prisons wataifuata Mwadui FC Jumapili.Baada ya kurejea nchini, Azam FC ilicheza mechi yake ya kwanza juzi kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi na kushinda 1-0 dhidi ya Mwadui FC, huku bao hilo pekee likifungwa na Kipre Tchetche dakika ya 18. | 4 |
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amevitaka vyuo vikuu kutumia nafasi zilizonazo za kitaaluma, kushirikiana na serikali katika kufanya utafiti wa kutosha dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto ili kumaliza tatizo hilo linalolikabili Taifa na dunia kwa ujumla.Aidha, amezitaka halmashauri zote nchini, kukamilisha uundaji wa kamati za ulinzi na usalama, zitakazoshughulikia matukio ya ukatili ya makundi hayo, sambamba na kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuratibu juhudi za kuzuia ukatili huo katika maeneo yao.Waziri Mkuu alitoa maagizo hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akifungua kongamano la Kitaifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto lililoandaliwa na Taasisi ya Utu wa Mtoto (CDF) na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali, zikiwemo taasisi zinazohusika na masuala ya kukemea ukatili huo.Alisema matukio ya ukatili dhidi ya watoto na wanawake nchini, bado yanazidi kujitokeza licha ya jitihada mbalimbali, zinazofanywa na serikali na wadau wengine za kuutokomeza na hivyo kuhitajika mbinu mbalimbali, zitakazosaidia kupata suluhu ya kudumu dhidi ya vitendo hivyo. Alisema kutokana na vyuo vikuu kuwa na wataalamu waliobobea katika masuala mbalimbali, ni vyema vikashirikiana na Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) kufanya utafiti huo utakaosaidia kuleta mabadiliko chanya katika jamii na hivyo kumaliza tatizo hilo.“Ukatili dhidi ya wanawake na watoto ni suala mtambuka linalohitaji nafasi ya kila mtu katika kulisimamia, nitoe rai kwa vyuo vikuu vyote zikatumia nafasi zilizonazo kufanya utafiti wa kutosha utakaosaidia kuleta mabadiliko dhidi ya suala hilo,” alisema Majaliwa. Alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizosaini na kuridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa na kikanda, yenye lengo la kuwalinda wanawake na watoto dhidi ya vitendo vyote vya ukatili huku ikitekeleza kwa vitendo Mpango wa Kitaifa wa NPA-VAWC2017/18 -2021/22 wenye lengo la kuzuia ukatili kwa wanawake na watoto katika nyanja zote.Alisema ili mpango huo na mikakati mingine iweze kuleta tija, hakuna budi kwa jamii nzima kubadili fikra na mitazamo hasi ya uendelezaji wa vitendo hivyo huku akilitaka jeshi la Polisi pamoja vyombo vya sheria kuhakikisha vinawalinda na kuwasimamia wanawake na watoto dhidi ya matukio yote yanayoonesha ukatili. Naye Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile, alisema wizara imekuwa ikiendeleza mikakati mbalimbali inayolenga kuimarisha na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.Dk Ndungulile alisema katika kutekeleza hayo, wamekuwa wakishirikiana na wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya dola, hatua iliyofanikisha kuanzishwa kwa madawati maalumu ambayo majukumu yake kutoa fursa kwa wanawake na waoto kutoa malalamiko yao. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utu wa Mtoto (CDF), Koshuma Mtengeti alisema lengo kuu la kongamano hilo ni kuwapatia fursa viongozi wakitaifa, watafiti, asasi za kiraia, wanataaluma, viongozi wa dini, wanaharakati wa haki za binadamu kutoka ndani na nje ya nchi kujadili hali halisi ya ukatili pamoja namna ya kuutokomeza.Alisema Tanzania inakabiliwa na kiwango cha juu cha ukatili kwa wanawake na watoto ikiwemo vipigo, ndoa za utotoni, mimba za utotoni, ukeketaji, unyanyasaji na hata ukatili wa kingono licha ya juhudi mbalimbali za kupinga vitendo hivyo bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka. Kongamano hilo linalomalizika leo, matarajio yake kuwa litaongeza uwajibikaji wa dhati wa wadau wote na hatimaye kuboresha upatikanaji na viwango vya huduma kwa waathirika wa vitendo hivyo vya ukatili na kuzithibitisha haki na heshima za wanawake na watoto wote nchini. | 3 |
RAIS John Magufuli amebainisha kuwa fedha zote zinazorejeshwa kutoka kwa wahujumu uchumi aliowaita mafisadi, zitatumika katika kutekeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo barabara na afya.Aidha, amewataka viongozi walioko madarakani wakiwemo mawaziri na viongozi wa chama tawala Chama cha Mapinduzi (CCM), kutangaza mafanikio yaliyopo katika maeneo yao, kwa kuwa serikali inatekeleza miradi ya maendeleo kwa fedha zake zikiwemo zinazorejeshwa na mafisadi.Rais Magufuli ameyasema hayo mkoani Katavi jana wakati akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Mlele baada ya kufungua Barabara ya Kanazi-Kizi-Kibaoni, ikiwa ni siku yake ya kwanza ya kikazi katika mkoa huo.Amesema kipindi cha nyuma, miradi mingi ilisuasua, ikiwemo ujenzi wa barabara kutokana na uhaba wa fedha. Lakini katika Serikali ya Awamu ya Tano, miradi mingi inatekelezwa kwa fedha za serikali kwa asilimia 100, zikiwemo zinazopatikana kutoka kwa mafisadi.Alisema barabara aliyoizindua mkoani humo ya kutoka Kanazi-Kizi-Kibaoni yenye urefu wa kilometa 76.6, iliyojengwa kwa thamani ya Sh bilioni 100, imejengwa kwa asilimia 100 na fedha za serikali, ambazo ni kodi za wananchi.“Kuzinduliwa kwa barabara hii sasa kimebaki kipande cha kutoka Kibaoni kwenda Stalike kilometa 71, naahidi kuwa barabara hii tutaitengeneza. Barabara hizi tunazijenga kuanzia Bukoba-Muleba, Biharamulo mpaka Nyakanazi, Kigoma mpaka Malagarasi, kote ni lami, tunataka kuunganisha wilaya ya Uvinza hadi Tanganyika, tunaenda mpaka Mpanda, Sikonge kilometa 356 na Stalike kilometa 36 ambako nitazindua kesho (leo),” amesisitiza.Amesema baada ya barabara hizo, imebaki eneo dogo la kilometa 71, ambazo aliziita mkia wa kondoo, ambazo nazo atazifagia kwa kuijenga kwa lami. “Fedha ipo, mafisadi wanarejesha, kwanini tuache kumaliza.Hela zinaingia za mafisadi, nyingine kidogo nitazileta hapa zimalize hii barabara,” alisema Rais Magufuli.Amesisitiza kuwa fedha zote zinazorudishwa na mafisadi, zitatumika katika masuala ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara za lami zinazounganisha Tanzania na nchi jirani. | 3 |
KAMERA 10 kati ya 16 zinazotakiwa kufungwa kwenye Daraja la Juu la Mfugale eneo la Tazara jijini Dar es Salaam, zimeshafungwa hadi sasa. Kamera sita zilizobaki, zitafungwa wakati wowote, baada ya nguzo kubwa inayosubiriwa kuletwa.Akizungumzia na gazeti hili kwa simu, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Mikataba cha Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Dar es Salaam, Abednego Lyanga alisema kazi hiyo, ilitakiwa iwe imekamilika mwishoni mwa mwezi uliopita.Lyanga alisema hata hivyo mkandarasi, Kampuni ya E 1, alishindwa kutokana na sababu za msingi ikiwa ni pamoja na kuchelewa kwa nguzo kubwa alizoagiza nje ya nchi kufika, zinazotumika kufunga kamera. “Hadi sasa kamera 10 zimeshafungwa, mbili zilifungwa mwishoni mwa Januari mwaka huu na kamera nyingine nane zimefungwa siku chache zilizopita na zilizobakia zipo ila kilichokuwa kinasubiriwa ni nguzo kubwa zilizoagizwa nje ya nchi,” alisema Lyanga.Alisema mkandarasi aliongezewa muda na mwezi huu atakabidhi kazi, baada ya kufunga kamera hizo na kufanya majaribio. Alisema katika daraja hilo na eneo hilo kwa ujumla, zinahitajika kamera 16 zitakazokuwa zikionesha matukio yote yanayoendelea hapo, na iwapo makosa ya usalama barabarani yatafanywa na madereva, itakuwa rahisi kuwabaini na kuchukua hatua.Lyanga alisema kamera 10 zilizofungwa, zinaendelea kufanya kazi sasa na zinaonesha matukio yote yanayoendelea darajani na zitaendelea kufanya kazi muda wote. Lengo la kuziweka ni kuhakikisha miundombinu ya eneo hilo, inakuwa salama, na kuwabaini madereva wanaokiuka sheria za barabarani ili vyombo husika viwachukue hatua. Agizo la kufungwa kamera hizo lilitolewa Septemba 27, 2018 na Rais John Magufuli wakati akizindua daraja hilo.Rais alisitiza kuwa kamera hizo, zitawabaini wananchi wanaoendesha vyombo vya moto bila kufuata taratibu, wakiwemo madereva walevi. Miezi mitatu baada ya agizo hilo la Rais Magufuli, utekelezaji ulianza kwa kamera mbili kufungwa mwishoni mwa Januari mwaka huu, kisha tena kamera nane zimefungwa hivi karibuni.Kinachosubiriwa ni nguzo kufungwa ili kamera sita zilizobaki zifungwe. Lyanga alisema gharama za uwekaji kamera hizo zote, umegharimu zaidi ya Sh milioni 100. Alisema kamera hizo zinaonekana mubashara na wanaweza kuangalia mwenendo mzima wa watumiaji daraja hilo. Daraja hilo lina urefu wa meta 425 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa meta 287 kila upande, na hivyo kufanya daraja lote kuwa na urefu wa kilometa moja. Ujenzi wake uligharimu Sh bilioni 106.9. | 3 |
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC, leo watakuwa katika Uwanja wa Uhuru kumenyana na Ndanda FC, mchezo ambao kama watashinda watazidi kujitengenezea nafasi nzuri ya kuutetea ubingwa wao kwani watabakiza pointi moja kuutwaa.Ili Simba ijihakikishie ubingwa inatakiwa kufikisha pointi 89 ambazo hata ikifungwa mechi zilizosalia bado itakuwa bingwa kutokana na hazina kubwa ya mabao iliyojiwekeza.Yanga inao uwezo wa kufikisha idadi hiyo ya pointi ikishinda mechi zake zote lakini lazima iwe na idadi kubwa ya mabao kuizidi Simba, jambo ambalo ni gumu.Simba ipo kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 85 ilizozikusanya katika michezo yake 34 ilizocheza ikifuatiwa na Yanga iliyo nafasi ya pili na pointi zake 83 ikiwazidi Simba michezo miwili.Ligi Kuu Tanzania inayoshirikisha timu 20 inaitaka kila timu kucheza mechi 38 ili kukamilisha msimu hivyo kama Simba watapata pointi nne katika mechi ya leo na inayofuata itakuwa mabingwa hata kabla haijamaliza mechi zake.Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza ambao ulipigwa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kumaliza dakika 90 kwa suluhu.Kocha wa Simba, Patrick Aussems amesema anajua mashabiki wa timu hiyo wanachokihitaji ambacho si kingine bali ni ushindi, atahakikisha wanafanya hivyo licha ya ratiba kuwabana kwa kuwalazimu kucheza mechi nyingi ndani ya kipindi kifupi.“Tunajua tuna muda mfupi ambao unatubana hata kufanya maandalizi ya nguvu, lakini kwa kuwa tunajua umuhimu wa mechi zetu zilizopo mbele yetu inatulazimu kupambana kivyovyote na kupata ushindi,” alisema Aussems. | 4 |
Na AGATHA CHARLES
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema matukio yaliyotokea hivi karibuni likiwamo la aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kutolewa bastola, yanaweza kubadili upepo wa Bunge linalotarajiwa kuketi siku chache zijazo.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, aliwaambia hayo waandishi wa habari jana waliotaka kufahamu mipango ya chama hicho katika kutumia mhimili wa Bunge kutokana na uwepo wa matukio ya uvunjaji wa sheria.
Katika hilo, Mnyika alisema Watanzania watarajie Bunge lijalo la Bajeti kuwaka moto.
“Sisi ndio tunaongoza Kambi Rasmi ya Upinzani na ambacho ninaweza kuwaambia Watanzania ni kwamba watarajie Bunge la Bajeti kuwaka moto juu ya utendaji wa Serikali. Sasa kuwaka moto namna gani na kuhusu nani ni masuala ambayo yataonekana katika hatua ya baadaye. Naamini safari hii haitakuwa wabunge wa Chadema, Ukawa pekee, naamini Bunge litakuwa kitu kimoja katika kuchukua hatua,” alisema Mnyika.
CHADEMA YANUNUA UGOMVI WA NAPE
Katika hatua nyingine chama hicho kimemtaka Rais Dk. John Magufuli ajitokeze waziwazi na kusema sababu za kumwondoa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
Pamoja na hilo, kimetaka Rais Dk. Magufuli aseme iwapo alitoa maelekezo kwa vyombo vya usalama waliovamia ofisi za Clouds Media Group na yule aliyemtolea bastola Nape alipokuwa akizuia asizungumze na vyombo vya habari juzi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, aliyezungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kuhusu ajenda mbili zilizozungumzwa katika kikao cha Kamati Kuu Maalumu ya chama hicho kilichoketi Machi 22 na 23, mwaka huu jijini Dar es Salaam.
“Ni vyema Rais akaeleza kwa kuwa taarifa za Ikulu hazikufafanua kwanini amemwondoa Nape. Aeleze waziwazi sababu za kumwondoa Waziri katika kipindi ambacho taarifa ya kamati iliyoundwa imetolewa ambayo imeeleza wazi makosa yaliyofanywa na mteule wa rais katika siku chache tu baada ya kumkingia kifua.
“Imeonekana matumizi mabaya ya wazi ya watumishi wa vyombo vya usalama ikiwamo waliovamia kituo cha Clouds kwa bunduki, aliyemtolea Nape bastola, rais ndiye msimamizi wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, awaeleze Watanzania iwapo askari na wanausalama hao wamefanya kazi kwa maelekezo yake,” alisema Mnyika.
Alisema kama sivyo ni hatua zipi ameelekeza zichukuliwe kwa wahusika wa mambo hayo.
Mnyika alisema chama hicho kinapinga mwenendo wa matumizi mabaya ya madaraka ikiwa ni pamoja na kulindwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na matukio ya hivi karibuni yanayogusa uhuru wa vyombo vya habari ikiwemo kuvamiwa kwa kituo cha Clouds Media Group pamoja na kitendo cha Nape kutolewa bastola.
“Uamuzi wa kumlinda Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa gharama hata ya kumwondoa Waziri wake ni wazi ni matumizi mabaya ya madaraka. Na matumizi haya mabaya ya madaraka yamejipenyeza sasa hayamhusu Rais tu pekee bali pia watendaji wake na vyombo mbalimbali,” alisema Mnyika.
Alisema nchi imeanza kuwa ya kipolisi na matumizi ya vyombo vya dola katika masuala ambayo havipaswi kutumika.
“Tunatoa pole kwa wanahabari kwa mambo hayo pamoja na Nape kwa haya yanayomkuta,” alisema Mnyika.
Alisema haki inapovunjwa mahali popote na kwa raia yeyote, wao kama chama hawasiti kutoa kauli ya kukemea.
Mnyika aliwataka Watanzania kuungana kupinga mabaya yanayofanywa na Serikali ili kulinusuru Taifa na hatari zinazoikumba na zitakazoendelea.
“Taarifa nilizonazo kutoka vyanzo vyangu serikalini ni kwamba, Rais ameamua kumlinda RC kwa sababu eti Chadema kupitia kwa Mwenyekiti Mbowe ilitoa msimamo wa kumtaka amchukulie hatua. Watu ndani ya Serikali wanasema kama atamchukulia hatua eti Rais ataonekana amekidhi matakwa ya Chadema,” alisema Mnyika.
Alisema chama chao kina wajibu wa kuikosoa Serikali iwapo haifanyi kazi sawa sawa na Rais anawajibika kwa wananchi na si Chadema.
Mnyika alikumbusha kuwa wakati walipotangaza Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta), waligusia kauli kuwa; anapoonewa yeyote, unapokuwa kimya, haki inapovunjwa kwa mtu mmoja ukadhani kwamba haikuhusu, ikaenda kuvunjwa kwa mtu mwingine ukanyamaza kimya ukadhani kwamba haikuhusu, ipo siku jambo litakukuta mwenyewe na hakutakuwa na mtu wa kupaza sauti kwa niaba yako.
Alisema kauli hii ilionekana kuwahusu upinzani pekee lakini hivi sasa imejidhihirisha tofauti kutokana na athari zinazojitokeza kwa raia, vyombo vya habari na baadhi ya wanaCCM.
CHADEMA MKOA WA DAR ES SALAAM
Chadema Mkoa wa Dar es Salaam kwa upande wao walisema wanaunga mkono msimamo wa Jukwaa la Wahariri (TEF), kwa kutoa maazimio ya kutofanya kazi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Katibu wa chama hicho mkoa, Henry Kilewo, alisema vyombo vya habari vinapaswa kuendelea kuwa imara na kusimamia kwenye misingi yao pasipo kuogopa au kupokea vitisho vyovyote kutoka ngazi yoyote huku akisema kuwa taifa haliongozwi kwa mihemko ya viongozi bali taratibu na sheria mbalimbali zilizowekwa. | 3 |
Kamishna Mkuu wa TRA nchini, Charles Kichere amesema katika taarifa yake kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mfanyabiashara atakayebainika kusafirisha bidhaa kwa magendo na kukwepa kodi nchini.Amewataka wafanyabiashara hao kuacha mara moja vitendo hivyo vinginevyo mali zao zote zitakazokamatwa na chombo kilichotumika kusafirisha au nyumba iliyohifadhi bidhaa hizo zitataifishwa na serikali kufidia ukwepaji kodi.Kichere alisema kukwepa kodi ni kosa la jinai kwa mujibu wa Sheria ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Mwaka 2005 na Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015.Alisema ukwepaji kodi husababisha mambo mengi ikiwemo kuikosesha serikali mapato.Kichere alisema ukwepaji kodi huhatarisha maisha ya walaji kwa kuingiza bidhaa ambazo hazijathibitishwa viwango vya ubora na usalama wake kupitia mamlaka husika kama Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), lakini pia huhatarisha uchumi na usalama wa nchi kwa sababu ya kuweza kuingiza vitu vya hatari kama silaha.TRA imewataka wananchi kutoa taarifa ya mfanyabiashara au kampuni inayojihusisha na magendo na kukwepa kodi kwa kupiga simu namba +255 22 2137638 au +255 784 210209.Hivi karibuni TRA ilitaifisha tani moja ya sukari na chumvi, majani ya chai mifuko 18, mirungi kilogramu 16, vifaranga vya kuku 5,000 na mayai kasha 416 mpaka wa Namanga, Arusha zikitokea Kenya kwa njia zisizo rasmi. | 5 |
Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Amaan usiku wa kuamkia jana, ulianza kwa Black Sailor kushinda bao la mapema lililofungwa na Ali Khalifa katika dakika ya nane.Kuingia kwa bao hilo kulizidisha kasi ya mashambulizi kwa timu hiyo huku wakikosa nafasi nyingi za wazi, lakini baadaye Black Sailor walionekana kudorora katika mashambulizi, hali iliyotoa mwanya kwa wapinzani wao kusawazisha na kuongeza bao.Jang’ombe Boys ambayo inafundishwa na kocha Issa Othman Amasha ambaye ni mchezaji wa Miembeni inayoshiriki Ligi Kuu ya Zanzibar, alijitahidi kutoa maelekezo kwa wachezaji wake na kufanikiwa kusawazisha bao hilo katika dakika ya 38 lililofungwa na Is-haka Said.Miamba hiyo iliendelea kushambuliana kwa zamu na kwenda mapumziko kila mmoja akiwa na haina bao.Kuanza kwa kipindi cha pili, kila upande ulijaribu kufanya mabadiliko huku mabadiliko yaliyofanywa na Jang’ombe yakiwa mwanga wa kuwawezesha kupata ushindi na kuvunja matumaini ya Black Sailor ya kucheza Ligi Kuu mwakani.Bao la pili ambalo liliwanyong’onyesha wapinzani wao lilifungwa na Khamis Mussa kwa shuti kali lenye umbali wa mita 24 kutoka kusini mwa uwanja huo, ambalo alilifunga kwenye dakika ya 69.Jang’ombe Boys na Black Sailor zote zimebakisha mchezo mmoja ambapo Black Sailor imeshacheza mechi mbili na kufungwa mechi zote, na ili isonge mbele itategemea na matokeo ya mchezo wa jana usiku ambao wapinzani wao watakaocheza nao mechi ya mwisho. | 4 |
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma iko katika mkakati kupata vyumba 52 vya madarasa kabla ya Februari 2, mwaka huu ili wanafunzi 2,610 waliofaulu na kukosa nafasi za kujiunga kidato cha kwanza wapate nafasi hiyo kusoma haraka.Akisoma ripoti mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge kabla ya kuanza ziara kukagua madarasa yatakapojengwa, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Hidaya Maenda alisema wamejipanga kumaliza upungufu huo.“Ili kuhakikisha mpango huo unafanikiwa, halmashauri imekaa na wakuu wa shule za sekondari zenye uhaba wa madarasa na kuweka mikakati kukamilisha miradi hiyo,” alisema.Maeda alisema mkakati ni kujenga madarasa mapya 20 katika shule 11 zenye upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa. Alisema tayari ujenzi umeanza katika shule hizo.Alisema mkakati huo unalenga kukamilisha madarasa 40 kati ya madarasa 52 yanayotakiwa. Ofisa Elimu wa Sekondari wa Jiji la Dodoma, Abdallah Membe alisema lengo ni kuhakikisha ujenzi wa majengo unakamilika katika muda uliopangwa ili wanafunzi waanze kusoma.Alisema idara ya sekondari imeanza kutekeleza shughuli zake kulingana na miongozo na mpango wa kazi wa idara shule zote 56 zenye jumla ya wanafunzi 19,205 wapate elimu. Katika wanafunzi 10,103 waliofanya mitihani darasa la saba mwaka jana, wanafunzi 5,428 walipangwa kujiunga na kidato cha kwanza awamu ya kwanza na wanafunzi 2610 wanasuburi kukamilishja madarasa waende.Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Mahenge baada ya kufanya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa alipongeza Jiji kutenga sh milioni 20 kwa kila sekondari yenye upungufu wa madarasa akawataka viongozi kushirikiana kukamilisha majengo wanafunzi wasome.Alitawaka watendaji wa mitaa na vijiji kuwahimiza wazazi kuwapeleka watoto wote shuleni kutokana na idadi ndogo ya wanafunzi walioripoti 1,951 hadi Januari 9 mwaka huu.Aliwataka wazazi kutowaondoa shule watoto waliofaulu ili waende kufanya kazi za ndani au kuozesha, wakati halmashauri ya jiji inafanya jitihada kuhakikisha wanapata nafasi kusoma. | 3 |
TAASISI ya Kuzuia na Kapambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Ruvuma imemfi kisha katika Mahakama ya Wilaya ya Mbinga Ofisa Mtendaji wa Kata ya Linda, Cosmas Nyoni akituhumiwa na makosa ya kuomba na kupokea fedha kwa njia ya rushwa.Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Ruvuma, Owen Jasson, mshitakiwa amefanya kosa kinyume cha kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007.Jasson alidai Agosti 3, 2018, Ofisi ya Takukuru Wilaya ya Mbinga ilipokea taarifa kuwa Nyoni kwa njia za rushwa Juni 29, 2018 aliomba Sh 550,000 kutoka kwa Zacharia Komba ili asimchukulie hatua na kumpelekea watu wa upekuzi nyumbani kwake ili kumpekua kwa makosa ya kujihusisha na ununuzi holela wa kahawa iliyopigwa marufuku ya magoma.“Siku hiyo mtuhumiwa alipokea fedha kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ni sehemu ya fedha alizoomba na siku ya Julai 4, 2018 alipokea tena fedha nyingine kiasi cha shilingi 250,000, pia ikiwa ni sehemu ya fedha alizokuwa ameomba,” alidai Jasson.Alidai baada ya kupokea taarifa hiyo, uchunguzi ulifanyika ambao ilithibitika kwamba ni kweli mshitakiwa alitenda makosa ya rushwa, hivyo Mei 17, mwaka huu, amefikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mbinga na kufunguliwa kesi ya jinai namba 41 ya mwaka 2019.Kulingana na Naibu Mkuu wa Takukuru, kesi hiyo imesomwa na Wakili wa Serikali, Chali Kadeghe mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbinga, Aziza Mbadjo. | 3 |
MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amesema ataendelea kutekeleza majukumu yake ya ofi sini kwani halmashauri hiyo imerejesha nywila (password) zilizokuwa zikitumika.Baada ya ofisi hizo kufungwa na kubadilishwa nywila na kuweka mpya, Mwita alisema halmashauri hiyo imerejesha nywila za zamani hivyo, ataendelea na kazi zake. Akizungumza na gazeti hili jana, Mwita alisema anachoamini kuwa yeye bado ni meya wa jiji hilo na kwamba kuna majukumu ya kuendelea kuyatekeleza.Mwita alisema kanuni ya 84 (1) ya halmashauri inaelekeza ili kumwondoa madarakani inapaswa kuwepo kura theluthi mbili ya wajumbe wote wa halmashauri na makosa yatakayosababisha kuondolewa yameainishwa kwenye kanuni hiyo kuwa ni rushwa, kutumia madaraka vibaya na kubaka.Alisema kanuni hizo hazikutimizwa katika kikao cha Januari 9, hivyo ataendelea kutekeleza majukumu ya umeya mpaka muda wake utakapokwisha.“Nilipewa barua Januari 10 ya kukabidhi ofisi na Mkurugenzi wa jiji, nilimjibu kuwa mimi ni meya halali kwa sababu akidi haikutimia siku ya kikao na nikamkumbusha kanuni zetu. Kuhusu ofisi tayari wameshabadilisha nywila ya kuingia hivyo naweza kuendelea na majukumu yangu,”alisema Mwita.Aliongeza kuwa wajumbe wa halmashauri ni kama wabunge ambao wakitaka kumuondoa Rais, Waziri Mkuu au Spika wanatakiwa kupata theluthi ya kura zote hivyo, kilichotokea ni kushindwa kutafsiri kanuni hiyo.Alisisitiza kuwa wajumbe walikuwa na uwezo mzuri wa kumuondoa kwenye nafasi hiyo endapo watakaporubuni mmoja wa wajumbe ili kukidhi akidi na kwamba siku 45 bado za kufanya hivyo zipo hivyo, wangepata kura 17 za kumtoa na kwamba wajumbe wasipohudhuria vikao mara tatu baraza hilo litavunjwa na kumkosesha nafasi.“Nimekuwa mwaminifu kwa kuleta maridhiano kwenye halmashauri yetu, sikuwahi kumvunjia mtu heshima wala kumdhalilisha mtu hivyo, haya ninayopitia nashangaa sana kwani nimedhalilishwa,”alifafanua Mwita na kuongeza: “Kama theluthi ingepatikana nisingeendelea kung’ang’ania kwa sababu ni ujinga tena ingefaa kukamatwa na vyombo vya dola lakini pia ningetakiwa kukata rufaa kwa Waziri husika wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na ingekuwa nafasi yangu ya mwisho lakini sijaondolewa,” Meya huyo alieleza kuwa akiendelea kupiga kelele atamzuia Rais kufanya kazi kwani anampenda na ni rafiki yake kwani ndiye aliyemfanya awepo hapo mpaka sasa.Kwa upande wa wakili wake, Hekima Mwasipu alisema Mwita akiondolewa madarakani kisheria hawezi kunufaika na mafao yake kwa sababu atakuwa amepoteza sifa kwa mujibu wa taratibu.“Endapo watamzuia kupata mafao yake, sisi tutafungua kesi nyingine mahakamani ili aweze kupata haki zake hata kama sio mwaka huu atazipata mwakani kwani bado ana sifa,” alisema. | 3 |
SERIKALI ya Finland inatarajia kutoa Euro 9.5 sawa na Sh bilioni 24/- kwa ajili ya mradi wa awamu ya pili wa Panda Miti Kibiashara.Mradi huo utakaodumu kwa miaka minne ni kwa ajili ya wakulima wadogo wa miti wa mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini.Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu aliagiza Idara ya Misitu na Nyuki ambayo ndiyo msimamizi mkuu wa mradi huo kwa niaba ya Wizara, iweke utaratibu wa kusimamia na itoe taarifa za mara kwa mara kuhusu maendeleo yake kwa wizara.Aliwataka wataalamu wote watakaotekeleza mradi huo, wafanye kazi kwa weledi mkubwa, kwa kuzingatia thamani ya fedha hiyo .Ametoa kauli hiyo Mafinga wilayani Mufindi mkoani Iringa alipokuwa akizindua awamu ya pili ya mradi huo.Awali serikali hiyo ya Finland katika mradi wa awamu ya kwanza, kati ya mwaka 2014 hadi mwaka 2018, ilitoa Euro milioni 19.5 sawa na Sh billioni 40.Kupitia uwezeshaji huo, hekta 12,000 za miti bora zimepandwa na zinamilikiwa na wananchi wapatao 9,030.Katika awamu hiyo ya kwanza, fedha hizo zilitumika kuanzisha kituo cha mafunzo ya misitu na Kiwanda cha Misitu cha Mafinga.Kituo hicho mpaka sasa kimeshatoa mafunzo kwa wakulima wapatao 8,555. Akizungumzia lengo la matumizi ya fedha hizo za awamu ya pili ya mradi, Kanyasu alisema fedha hizo zitatumika kuwajengea uwezo wakulima wa miti na wajasiriamali wadogo na wa katiAlisema fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kupambana na matukio ya moto na kuongeza ubora wa mazao ya misitu yaliyo kwenye mnyororo wa thamani.Katika hatua nyingine, Naibu Waziri huyo aliishukuru Finland kwa kufadhili mradi mwingine wa kuongeza mnyororo wa thamani kwa mazao ya misitu uitwao FORVAC, unaotekelezwa na wizara katika wilaya kumi za mikoa ya Tanga, Dodoma, Lindi na Ruvuma.Alisema sekta ya misitu nchini isingefika hapa ilipo leo, kama hapangekuwepo msaada wa wananchi wa Finland. Balozi wa Finland nchini Tanzania, Riita Swan alisema nchi yake imeatoa fedha hizo kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wadogo wa miti ili wajikwamue na umasikini.Kwamba Finland inataka kuona wakulima wadogo wa miti, wanajengewa mazingira mazuri ya kushiriki katika shughuli za kuendeleza misitu kibiashara. | 5 |
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa alitoa rai hiyo jana alipowatembelea wafanyabiashara hao maarufu kama wamachinga, kwenye soko la Rehema Nchimbi Complex lililopo mjini hapa kwa lengo la kukagua mazingira ya kufanyia biashara sokoni hapo.Galawa alisema biashara ya uchuuzi haiwaletei faida na mafanikio yanayohitajika badala yake inawafaidisha zaidi wazalishaji wenye viwanda, wengi wao kutoka nje ya nchi.“Lazima mbadili mtazamo na kujikita katika kuanzisha viwanda vidogovidogo ili kuingia katika biashara ya uzalishaji bidhaa na usambazaji wake ambayo itawaletea mafanikio makubwa kiuchumi,” alisema.Pia aliwataka wamachinga kujitathmini kila mmoja anavutiwa na kufanya uzalishaji wa bidhaa zipi huku wakichambua fursa zinazopatikana mkoani Dodoma.Alizitaja baadhi ya fursa zilizopo mkoani Dodoma ni pamoja na uwepo wa viwanda vya nyama hivyo kuna nafasi nzuri ya kuanzisha viwanda vidogo vya kutengeneza bidhaa za ngozi kwa kuwa malighafi ya ngozi ya asili ya wanyama itapatikana kwa urahisi kutoka kwenye viwanda hivyo vya nyama.Aliwahakikishia upatikanaji wa soko la bidhaa zao endapo watajitahidi kutengeneza bidhaa zenye ubora. | 5 |
Lipuli itaikaribisha Simba kwenye uwanja wake wa nyumbani Samora ikiwa imetoka kuifunga Singida United bao 1-0 ambapo Matola anasema ushindi huo umewapa morali ya mechi dhidi ya Simba.Matola, ambaye aliwahi kuichezea Simba na kuwa kocha wa timu hiyo pamoja na zile za vijana, amesema wanataka kuwa timu ya kwanza kuifunga Simba msimu huu bila kujali uhusiano uliopo kati yake na klabu hiyo kongwe.Simba ndio timu pekee ambayo haijapoteza mechi hata moja kati ya mechi 24 ilizocheza.Inaongoza msimamo kwa pointi 58.“Mwisho wa mchezo ndiyo mwanzo wa mchezo mwingine, tunajipanga kwa ajili ya Simba tunajua ni timu ambayo haijafungwa kwenye ligi lakini sisi tunataka kuwa timu ya kwanza kuifunga Simba,” amesema Matola.Matola alisema mchezo dhidi ya Singida United ulikuwa mgumu licha ya kupata ushindi kwenye uwanja wa nyumbani Samora, Iringa.“Mechi ilikuwa ngumu sana kwa sababu ukiangalia Singida United ni miongoni mwa timu ngumu kwenye ligi, timu ambayo imewekeza lakini nawapongeza wachezaji wangu kwa sababu wamefanya kitu ambacho tumewatuma na kila mwana Iringa alitaka wakifanye,” alisema Matola.Bao pekee kwenye mchezo huo lilifungwa na Malimi Busungu na kuifanya Lipuli kufikisha pointi 31 kwenye nafasi ya nane. | 4 |
TIMU ya taifa ya Soka ya Wanawake ya Tanzania Bara, ‘Kilimanjaro Queens’ jana ilimaliza kwa kishindo hatua ya makundi ya Mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) baada ya kuifunga Zanzibar mabao 7-0.Mchezo huo wa kukamilisha ratiba baada ya Zanzibar kuwa tayari ilishatolewa kutokana na kufungwa mabao yote, Kilimanjaro Queens walitawala muda wote na kulishambulia lango la wapinzani kama nyuki.Mchezaji Deonisia Minja aliifungia Kilimanjaro Queens mabao mawili, katika dakika ya 26 na 55, huku Diana Msewe aklifunga bao katika dakika ya 30 huku Philomena Kizima alifunga katika dakika ya 69 kwa shuti kali.Mabao mengine ya Kili Queens yalifungwa na Asha Rashid katika dakika ya 83 na 85, huku Anastazia Katunzi akifunga la saba katika dakika ya 87 na kuwafanya wenyeji kuondoka na ushindi mnono wa mabao 7-0.Stars imefunga magoli 20 katika michezo yake mitatu huku golikipa, Zubeda Mugunda pamoja na safu yake ya ulinzi wakiwa hawajaruhusu goli hata moja huku Zanzibar ikibeba kapu la magoli 17 bila kufunga goli hata moja katika michezo yake yote mitatu.Katika mchezo wa awali jana, Burundi waliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sudan Kusini na kuifanya Burundi kutinga hatua ya nusu fainali na kuzifuata Kilimanjaro Queens, Kenya na Uganda.Kundi B mechi zake wanamaliza kesho kwa Kenya kucheza dhidi ya Uganda na hapo ndipo atajulikana mpinzani wa Kilimanjaro Queens kwani timu hizo kila moja ina pointi 14 na imefungwa bao moja tu. Mshindi wa pili wa Kundi B ndiye atakayecheza dhidi ya Kilimanjaro Queen wakati mshindi wa kwanza atacheza na Burundi, ambaye ndiye mshindi wa pili wa Kundi A. | 4 |
Mwandishi wetu, Tanga WAFANYABIASHARA wa Mkoa wa Tanga, wamesema hawaoni shidakulipa kodi baada ya kuona utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleoinayofanywa na Rais Dk. John Magufuli kupitia kodi zao. Hayo yalizungumzwa na wafanyabiashara wakati wa kampeni ya elimukwa mlipakodi inayoendelea mkoani humo ambako maafisa wa Mamlakaya Mapato Tanzania (TRA) kutoka Makao Makuu kwa kukishirikiana namaafisa wa TRA mkoa wa Tanga. Maafisa hao waliwatembelea wafanyabiashara kwenye maduka yaoyaliyopo barabara za namba jijini Tanga kwa lengo la kuwaelimisha nakuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati.Sambamba na hilo, maafisa hao pia waliweza kusikiliza kerozinazowakabili wafanyabiashara mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusikiliza maoni yao kama mpango wa kutengeneza mazingira rafiki kati yao naTRA.Thabiti Salimu ambaye ni mfanyabiashara wa Ukwaju wa jumla na rejarejakatika eneo la barabara za namba amesema kuwa, atamshangaamfanyabiashara atayekwepa kulipa kodi hususani katika kipindi hikiambacho wameshuhudia miradi mingi ikitekelezwa kupitia kodi zao. “Rais Magufuli anatumia kodi zetu vizuri, tunaona utekelezaji wa miradimingi ya maendeleo hivyo lazima tuendelee kulipa kodi la sivyo kazi yautekelezaji wa miradi hii itakwama,” alisema Salimu. Naye Dina Mbenu, mfanyabiashara wa vipuli vya pikipiki amesema kuwa,ikiwa wafanyabiashara watakwepa kulipa kodi watasababisha madhara yakiuchumi na kuathiri jitihada za serikali za kuboresha miundombinuikiwemo barabara. Amesema hatua ya maafisa wa TRA kuwatembelea kwenye maduka yaokwa lengo la kuwahamasisha kulipa kodi na kusikiliza kero na maoni yaoinawasaidia kutopoteza muda kwenye ofisi za TRA wakisubiri kuhudumiwa. Kwa upande wake Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi Julius Mjenga amesemazoezi la kuwatembelea wafanyabiashara ni endelevu na kabla ya kufanyikaTanga, zoezi hilo limeshafanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza,Mbeya na Morogoro. Amesema lengo la kufanya hivyo ni kutoa elimu ya kodi, kuwakumbushawafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati, kusikiliza maoni yao pamoja nachangamoto kwa ajili ya kuzitatua.Naye Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure, aliwaombawafanyabiashara kuunga mkono zoezi linalofanywa na maafisa wa TRA lautoaji elimu ya kodi, kusikiliza maoni na changamoto zao kwa kuwa zoezi hilo linalenga kuboresha huduma kwa mlipakodi.“Niwaombe wafanyabiashara wote mkiwaona maafisa wanatembelea,msifunge maduka, wapokeeni na kuwapa ushirikiano kwa kuwa wanalengakuwaelimisha na kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili kwenyebiashara zenu ambazo kwa pamoja tunaweza kuzitafutia ufumbuzi,”alisema Owure. Amesema zoezi hilo la utoaji wa elimu ya kodi kwa wafanyabiasharamkoani humo linatarajiwa kumalizika Juni 30, 2020 na kwamba lengo likiwani kutaka kuwafikia wafanyabiashara wengi mkoani hapo. | 5 |
Na RENATHA KIPAKA – BUKOBA MIRADI tisa ya vyanzo vya maji katika wilaya nne za Mkoa wa Kagera, vimepungukiwa maji kwa asilimia kubwa hali inayofanya wananchi wa wilaya hizo kupata maji kwa mgawo na wengine kuyafuata umbali mrefu. Akizungumza na MTANZANIA juzi, Mhandisi wa Mkoa wa Kagera, Vitus Exsavery, alisema vyanzo rasmi na visivyo rasmi vilivyoko katika vijiji vya wilaya za mkoa huo vimekauka na baadhi vimepungua maji kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi. Alisema upungufu wa upatikanaji maji kwa wananchi hao, unasababisha mgawo baada ya mahitaji ya lita zilizokuwa zikihudumia saa 24 kutokuweza kutoka tena na wilaya ambazo zimepungukiwa maji kabisa ni Biharamulo ambayo ilikuwa na chanzo cha bwawa moja lililokuwa likihudumia wakazi wote limekauka na kubakiwa na tope. “Mpaka sasa tuliamua kuwagawia maji kwa saa, kwa mfano lita 18,000 zilikuwa zikitoka kwenye chanzo chenye uwezo wa kugawia zaidi ya vijiji vitatu, nyakati hizi maji yanatoka kidogo sana yasiyoweza kuwagawia wote kama ilivyokuwa imezoeleka,” alisema Exsavery. Alisema Wilaya ya Bukoba ilikuwa ikihudumia vijiji vitatu cha Bonakilovyo, Kitaya, Kabumbilo kutoka kwenye chemichemi kusambaza katika vijiji hivyo imepungua kwa kiwango cha asilimia 80, wananchi hupata maji kwa mgawo. Alisema katika miradi miwili iliyojengwa kwenye kata ambazo hazipati maji ya Buwasa hutoa maji katika vyanzo vya Kijiji cha Bunkango kilichopo Kata ya Nshabya na Bulibata ambao hutoa maji kwenye chanzo cha Nyamganja. | 3 |
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA), ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Chama alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.Alisema makandarasi walianza kazi jana kuweka nyasi hizo bandia na kuongeza kuwa baada ya Ligi Kuu Tanzania Bara kusimama kupisha mechi za Kombe la FA, mechi za Kagera Sugar zijazo itachezewa katika uwanja huo.Chama alisema kutokana na uwanja huo kubandikwa nyasi itakuwa kivutio hata kwa timu nyingine kuutumia uwanja huo katika shughuli mbalimbali za kimichezo zitakazokuwa zinaendelea hapa nchini.Alisema kuwa baada ya uwanja huo kukamilika utasababisha kukuza uchumi wa Manispaa ya Bukoba maana mashabiki wa mpira watakuwa wengi tofauti na ilivyokuwa awali.Pia alisema kutokana na mabadiliko ya uwanja huo hautatumika katika shughuli nyingine kama kuingiza magari au gwaride maana umebadilika sio kama ulivyokuwa mwanzo.Kwa upande wake Diwani Mteule wa kata ya Miembeni ulipo Uwanja wa Kaitaba, Richad Mwemezi alisema amepata faraja kubwa sana kwa tukio hilo la kuwekwa nyasi bandia maana limekuwa ni tukio la kihistoria. | 4 |
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara Simba leo watakuwa wenyeji wa Mbao ya Mwanza katika mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro.Mchezo huo ni wa kisasi kwa Simba baada ya raundi ya kwanza kupoteza kwa bao 1-0 kwenye uwanja wa CCM, Kirumba, timu pekee iliyowafunga wekundu hao msimu huu. Timu hizo zinakutana Simba ikiwa kwenye kasi baada ya kucheza michezo 21 na kufikisha pointi 54 ikishika nafasi ya tatu, ikishinda michezo 17 na kupata sare tatu.Aidha, ubora wa kikosi hicho cha Msimbazi hasa katika safu ya ushambuliaji ni hatari kwa mabeki wapinzani kutokana na kasi ya ufungaji ikiongozwa na Meddie Kagere aliyeifungia timu yake mabao 13 akishika nafasi ya pili nyuma ya Salum Aiyee wa Mwadui mwenye mabao 16.Mbao ni timu inayoonekana kuwazidi ujanja timu vigogo hasa zinapokuwa kwenye uwanja wao wa Kirumba lakini wanapotoka nje hupigika. Timu hiyo ilianza kuyumba hivi karibuni kiasi cha kushindwana na makocha wawili waliochana nao akiwemo Amri Said na Ally Bushiri. Wababe hao wa Simba na Yanga wanashika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi baada ya kucheza michezo 30, kushinda tisa, sare 10 na kupoteza 11 wakiwa na pointi 36 walizofungana na timu nyingine tano.Mchezo huo utakuwa mtihani wa kwanza kwa Kocha mpya wa kikosi hicho Salum Mayanga aliyekabidhiwa timu hiyo hivi karibuni. Huenda ukawa ni mchezo mgumu hasa kwa Mbao kwani wekundu hao wanataka kuendelea na rekodi yao ya kushinda ili kujiweka karibu na utetezi wa taji la ligi. Lakini pia, ikiwa Mbao itapoteza itakuwa hatarini kuwa kwenye ukanda wa kushuka daraja kama tu wengine waliofungana kwa pointi watashinda michezo yao ijayo. | 4 |
Alisema mradi huo wa nyumba unajengwa katika eneo la Iyumbu, karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma. Alisema hatua hiyo itapunguza uhaba wa nyumba za makazi na biashara katika manispaa ya Dodoma, kwa kuwa miradi mingine ya nyumba za biashara itajengwa katika eneo Meledeli.Akifafanua, Gambalagi alisema NHC itatekeleza miradi miwili ya nyumba za gharama nafuu katika Halmashauri za Chamwino na Bahi ambapo zaidi ya nyumba 50 za kuuza zitajengwa katika mwaka huu wa fedha.Alisema katika kutekeleza miradi hiyo NHC itajenga nyumba za kuuza kwa zile halmashauri zitakazoonesha zina mahitaji na utayari wa kulipia au kuwepo kwa soko la nyumba zitakazojengwa.Gambalagi alisema kwa nyumba za kupangisha, shirika linaendelea kuzifanyia matengenezo makubwa nyumba zake inazomiliki katika Manispaa ya Dodoma. Alisema hivi karibuni, shirika lilibadilisha madirisha ya kizamani na kuweka madirisha ya kisasa kwenye nyumba zake zilizopo eneo Mpwapwa ya zamani na zile zilizoko barabara ya Iringa.Alisema shirika pia limesaidia vijana kwa kila halmashauri ya wilaya, mkoani hapa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana ili kuwapa ajira na kuwaondolea umasikini. | 5 |
BAADA ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kumtaka Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad, kufi ka mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kujibu tuhuma za kulidhalilisha Bunge kuwa ni dhaifu, wanasheria na wasomi wamefunguka kuhusu suala hilo.Ndugai alivieleza vyombo vya habari jijini Dodoma juzi kuwa CAG pamoja na Mbunge wa Kawe jijini Dar e s Salaam, Halima Mdee (Chadema) ambaye aliunga mkono kauli ya CAG kuwa Bunge ni dhaifu, wanapaswa kufika mbele ya Kamati hiyo Januari 21 na 22, mwaka huu. Gazeti hili jana liliripoti kuwa Desemba 30 mwaka jana, Profesa Assad wakati akifanya mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, alisema kuwa Bunge la Tanzania ni dhaifu, kwa kuwa limeshindwa kuzifanyia kazi ripoti za ufisadi, zinazotolewa na ofisi yake.Kauli hiyo ya CAG, ilimuibua Spika Ndugai aliyedai kuwa CAG ndiye anayepotosha, kwa kuwa haiwezekani aiseme nchi yake vibaya anapokuwa nje ya nchi, hivyo kuagiza CAG na Mdee kufika kuhojiwa na wasipotekeleza wito huo, hatua nyingine zitachukuliwa dhidi yao. Kutokana na hali hiyo, Wakili wa Kujitegemea, Albert Msando, alilieleza gazeti hili jana kuwa wakati CAG anatekeleza wajibu wake kisheria, hawezi kuhojiwa kwa jambo lolote na mtu yeyote, kwa kuwa sheria inamlinda.Hata hivyo, alisema kwa upande mwingine wa shilingi, Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, inaeleza kuwa mtu yeyote, bila kujali nafasi yake, hapaswi kulidharau au kulikashifu Bunge na akifanya kosa hilo, Spika anaweza kumuita ili kuhojiwa na kamati hiyo. Ili kujua nguvu aliyonayo CAG ya kulindwa na sharia, lakini pia na nguvu iliyonayo Bunge ya kumhoji mtu yeyote anayelidharau, gazeti hili lililazimika kutafuta tafsiri ya kisheria na utawala bora juu ya muktadha huo.Msando alisema katika suala hilo la Spika na CAG, kilichotakiwa kuangaliwa kwanza ni tafsiri ya neno ‘dhaifu’ kama ni kweli neno hilo linalidhalilisha Bunge au la. Alisema kama tafsiri ambayo ilipaswa kuangaliwa, ingethibitisha ni kweli neno hilo linalidhalilisha Bunge, basi ndipo Bunge lingekuwa na sababu ya kumwita CAG kwa mahojiano.“Sasa swali ni kwamba nani mwenye mamlaka kisheria ya kutafsiri neno ‘dhaifu’ kama linalidhalilisha Bunge au la? Hapa kingepaswa kiundwe chombo kingine huru cha kutoa tafsiri na si Bunge lenyewe ambaye ni mlalamikaji kufanya kazi hiyo. Bunge haliwezi kuwa mlalamikaji na mwamuzi lenyewe, na katika kipengele hiki, sheria iko kimya”alieleza Msando. Kwa mujibu wa Msando, kwa kuwa CAG alitoa kauli hiyo wakati ambao hakuna Bunge linaloendelea, hajalidhalilisha Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 24 cha Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.“Spika alipaswa kulipeleka jambo hili kwenye mamlaka iliyomteua CAG yaani Rais na kulalamika kuwa amelidhalilisha Bunge katika vyombo vya habari, ndipo mamlaka iliyomteua CAG ingepima na kutoa uamuzi,” alieleza Msando. Wakili huyo alisema kuwa Spika alipaswa kumfikishia wito huo CAG kimaandishi, akiweka hoja zote ambazo CAG anatakiwa kuzitolea ufafanuzi katika utetezi wa kauli yake ; na si kueleza jambo hilo kwenye vyombo vya habari. Alisema hata kama CAG atakwenda kuhojiwa, bado Bunge haliwezi kisheria kumshauri Rais atengue uteuzi wake, ila linachoweza kufanya ni kutoa karipio tu.Msando alisema kwa kuwa Bunge na CAG wanafanya kazi kwa karibu na kwa kushirikiana, kama itaonekana jambo hilo linaleta ukakasi katika kutimiza majukumu yao, ndipo sasa Rais mwenyewe anaweza kuamua ama aendelee naye au amtoe au yeye CAG mwenyewe, aamue kwa hiari yake kujiuzulu kutokana na hali ya kutoaminiana kati yake na Bunge. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye ni Mtaalamu wa Sayansi ya Siasa, Dk Benson Bana, alisema kuwa uamuzi wa Bunge kumwita CAG na kutaka kumhoji ni sahihi, kwa kuwa kauli yake ya kwamba Bunge ni dhaifu, aliitoa akiwa nje ya ofisi yake.Alisema CAG anapaswa kuwa makini na kauli zake, kwa kuwa yeye ni sehemu ya serikali, hivyo ana wajibu wa kuhakikisha mwenendo, kauli na tabia yake vinaendana na dhana ya utawala bora, ikiwemo kuheshimu mihimili mingine ya dola. Mihimili ya dola ni Mahakama, Bunge na Utawala (Serikali). “Kwa kweli kauli ya kusema Bunge ni dhaifu inachefua. Kauli kama hii inapaswa kutolewa mahali sahihi na si hadharani kama hivyo, kwa hiyo ni sahihi kwa Spika Ndugai kumwita ili ahojiwe ili kujua kauli yake ina mwelekeo gani, na CAG si kiongozi wa kwanza kuitwa na Bunge kwa sababu hata Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alishawahi kuitwa na kuhojiwa na Bunge,”alieleza Dk Bana.Majukumu ya Kamati ya Haki na Maadili ya BungeKanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Januari 2016 Nyongeza ya Nane Kifungu cha 4 (1) (a) na (b), kinaeleza kuwa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itatekeleza majukumu yake kwa: Kuchunguza na kutoa mapendekezo kuhusu masuala yote ya haki, kinga na madaraka ya Bunge, yatakayopelekwa na Spika ; na kwamba itashughulikia mambo yanayohusu maadili ya Wabunge yatayaopelekwa na Spika.Kamati hiyo itakapokamilisha kushughulikia jambo husika, Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika kwa maandishi kwamba Kamati imemaliza kujadili jambo husika na Spika baada ya kupokea taarifa hiyo, ataagiza iwekwe kwenye Orodha ya Shughuli za Bunge kwa ajili ya kuwasilishwa na kujadiliwa bungeni.Kinga ya CAG kikatibaHali ikiwa hivyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Ibara ya 143 (6) inasema kwamba, katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2), (3) na (4) ya ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali.Lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo, hayataizuia Mahakama kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au sivyo.Katiba inavyoweza kumwondoa CAGKwa mujibu wa Ibara ya 144 (1), CAG atalazimika kuacha kazi yake atakapotimiza umri wa miaka sitini au umri mwingine wowote, utakaotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge.Na Ibara ya 144 (2) inaeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu anaweza kuondolewa katika madaraka ya kazi yake, kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake, ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote, au kwa sababu ya tabia mbaya, au kwa kuvunja masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; na hataweza kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya 4 ya ibara hii.Nafasi ya Rais katika kumwondoa CAGRais ana mamlaka kikatiba ya kumwondoa CAG kwa mujibu wa Ibara ya 144 (3)(a) (b). Ibara hiyo inasema kuwa iwapo Rais ataona kwamba suala la kumwondoa kazini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kwa mujibu wa masharti ya ibara hii linahitaji kuchunguzwa, basi atateua Tume Maalum ambayo itakuwa na Mwenyekiti na Wajumbe wengine wasiopungua wawili. Kwa mujibu wa ibara hiyo, Mwenyekiti na walau nusu ya wajumbe wa Tume hiyo wanapaswa kuwa watu ambao ni Majaji au watu waliopata kuwa Majaji wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufani katika nchi yoyote iliyomo kwenye Jumuiya ya Madola.Ibara hiyo inafafanua kuwa Tume hiyo itachunguza shauri lote na kisha kutoa taarifa kwa Rais kuhusu maelezo ya shauri lote na itamshauri Rais kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, aondolewe kazini kwa mujibu wa masharti ya ibara hiyo kwa sababu ya kushindwa kufanya kazi kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya. | 3 |
VIONGOZI wa mila ya jamii ya kifugaji ya kimasai maarufu kwa jina la Laigwanani kutoka katika wilaya nane za mikoa ya kanda ya kaskazini na wafugaji zaidi ya 150, wamemzawadia Rais John Magufuli ngo’mbe dume ikiwa ni ishara ya kuongoza nchi kizalendo na kusimamia haki kwa wanyonge.Viongozi hao wamejitokeza katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexinder Mnyeti na kutoa zawadi hizo ambazo kwa mujibu wao Rais amekuwa mstari wa mbele kukutea maslahi ya wanyonge hususani wafugaji walioteseka kwa miaka mingi ndani ya nchi yao.Mmoja wa viongozi wa mila, Jackson Ole Teteyo alisema kuwa zawadi ya ng’ombe huyo dume ni alama ya uzalendo.Mara ya mwisho kwa viongozi wa mila kutoa zawadi ya dume huyo ilikuwa mwaka 1986 kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ushujaa wa kuiongoza nchi kizalendo bila ya kumuonea haya kiongozi anayeshindwa kuiongoza serikali yake.Teteyo alisema kuwa Rais alikabidhiwa dume huyo kupitia mwakilishi wake Mkuu wa Mkoa, Mnyeti aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Babati, Elizabeth Kitundu katika shughuli ya utoaji wa zawadi hiyo iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara.Alisema wafugaji wameguswa na jinsi Dk Magufuli anavyofanya kazi kwa kuwajali wanyonge hususani wafugaji na kuwaamrisha watendaji wa serikali kuiongoza nchi kwa maslahi ya wananchi na sio maslahi yao binafsi.Alieleza kuwa aina ya uongozi wa Rais Magufuli unafanana na uongozi wa Baba wa Taifa na ndio maana Malaigwanani wameguswa na uongozi huo na kuamua kutoa zawadi pekee ya dume la ng’ombe.Kiongozi huyo alisema kuwa kitendo cha kusitisha uhamishwaji wa vijiji 366 vilivyopo karibu na hifadhi za taifa ni uamuzi ulioungwa mkono na kila mfugaji kote nchini na viongozi wa mila wameaswa kuheshimu kauli hiyo na kusubiri utekelezaji wa maagizo hayo. | 3 |
KAMATI ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imeipa miezi mitatu Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalumu wa upotevu wa zaidi ya Sh bilioni 3, fedha za miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyangh’wale mkoani Geita.Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Abdallah Chikota ametoa agizo hilo jijini Dodoma baada ya kukutana na uongozi wa wilaya hiyo kuhusu hoja za ukaguzi za CAG kwa mwaka wa fedha2017/18.Chikota alisema kwa kiasi kikubwa ripoti waliyopelekewa na ofisi ya CAG imejaa ubadhirifu na kwamba kamati hiyo imeshindwa kuhoji watendaji hao wa halmashauri kutokana na kuwa watendaji wengi ni wapya.Kutokana na ubadhirifu huo, LAAC imeagiza kufanyika kwa ukaguzi maalumu ili kuwabaini watumishi wengine waliohusika katika wizi huo.“Ofisi ya CAG iende kufanya ukaguzi maalum kwenye halmashauri hii maana pamoja na kwamba kuna watumishi ambao wapo ndani na wengine kesi zao zipo mahakamani, tunaoana bado kuna wengine wapo nje sababu CAG alizuiliwa kufanya ukaguzi ambao utaweza kusaidia kuwajumusiah na wengine walioshiriki,” amesema.Akibainisha baadhi ya maeneo ambayo hesabu zake zinaonesha kuna ubadhirifu, Chikota alisema kuna vitabu 50 vya kukusanyia mapato taarifa yake haikuwasilishwa kwa wakaguzi.Alisema pia hati za malipo zenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1, sambamba na kuwepo kwa malipo yasiyo na viambatanisho yenye thamani ya Sh milionbi 339.7.Chikota alisema pia taarifa hiyo inaonesha kuwepo uhamisho wa fedha bila kuonesha shughuli zilizofanyiwa kiasi cha Sh bilioni 1.7.“Fedha zinaonesha zimefanyiwa uhamisho, lakini wakaguzi wakifuatlia hakuna shughuli ambazo zimefanya,” aliongeza.Aliongeza, “hata walipojaribu kukagua utekelezaji wa miradi nako kuna changamoto na kumbwa ikiwa ni ucheleweshwaji wa kukamilika kwa miradi ya maendeleo pamoja na kuonekana fedha kutolewa.” Chikota alisema katika sekta ya afya, serikali ilitoa kiasi cha Sh milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya, taarifa inaonesha fedha hizo hazipo na kituo hakijajengwa.Alisema pia fedha zilizotolewa kwa ajili ya Mradi wa Elimu wa EP4R kiasi cha Sh milioni 576 taarifa hiyo inaonesha zimetumika nje ya malengo yaliyokusudiwa.Chikota alisema pia katika mradi wa maji taarifa za kwenye kitabu zinaonesha kuwepo kwa salio la Sh milioni 74.1, lakini taarifa ya benki inaonesha kiasi cha Sh milioni 71.1 haipo.“Si hivyo tu, hata fedha ambazo zinaoneshwa zimeliwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu wa maji, kuna hati za malipo zenye thamani ya shilingi milioni 134.5 hazikuwasilishwa kwa wakaguzi,” amesema.Amesema watumishi hao wanaonesha kuwa pia walipewa kiasi cha Sh billion 1.9 kwa ajili ya miradi ya maendeleo lakini ni Sh milioni 700 pekee ndizo zilizotumika huku zingine zikiteketezwa.“Kwa mazingira haya kamati tusiendelee kuwahoji, CAG tunakupa muda mfupi sana wa miezi mitatu, kwa kufanya hivyo kutafanya kujua wahusika kulingana na kila hoja moja,” amesema.“Haiwezekani tukafumbia macho suala hili maana hata kama kuna watendaji wapya kwa sasa hatuwezi kuwasifia wakati wizi bado unaendelea kufanyika kama kawaida.”Naibu Waziri Tamisemi, Mwita Waitara alisema watachukua hatua kadiri Kamati ya Bunge itakavyowaagiza mara baada ya uchunguzi kukamilika. | 3 |
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dk Arnold Kihaule ametua mkoani Morogoro akiwa na vitambulisho vya taifa 24,010.Alitua Morogoro jana ili kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kufika mkoani humo na kukaa siku tatu, ili aweze kutatua tatizo la upatikanaji wa vitambulisho hivyo kwa wananchi. Rais Magufuli alimpa agizo hilo kwa njia ya simu juzi, baada ya wananchi kutoa malalamiko yao juu ya ugumu wa kupata vitambulisho hivyo. Alizungumza nao eneo la Msamvu mjini Morogoro, akiwa njiani kuelekea Dodoma.Walimueleza Rais kuwa wanashindwa kusajili namba zao za simu, kwa kuwa hawana vitambulisho na kwamba huduma hiyo haipatikani kwa urahisi.“Nimefika leo asubuhi (jana) baada ya kupokea maelekezo ya Rais nije Morogoro ili kutatua changamoto mbalimbali za wananchi kuhusu suala la utambuzi na usajili wa kupata vitambulisho vya taifa na nimekuja na vitambulisho 24,010,” alisema Dk Kihaule.Alisema vitambulisho vingine 78,081, vililetwa mkoani Morogoro Novemba 16, mwaka huu na sasa vinafanyiwa utaratibu wa kufikishwa katika kata, vijiji na vitongoji ili viwafikie walengwa. Kwamba vitambulisho vingine 17,400 tayari vimesambazwa kwenye wilaya zote za mkoa huo hadi ofisi za kata, vijiji, mitaa na vitongoji. Aliwataka wananchi kwenda kuangalia namba zao na kuchukua vitambulisho hivyo.“Maofisa usajili wote wa wilaya za mkoa wa Morogoro wahakikishe wanasambaza namba za vitambulisho na vitambulisho katika ngazi za kata, kijiji, kitongoji na mtaa ili wananchi waweze kufika kuangalia namba zao na vitambulisho ili wavichukue kwa utaratibu uliopangwa,” alisema Dk Kihaule.Alisema tayari ameshakutana na uongozi wa mkoa wa Morogoro ili kuwezesha kuwa na utaratibu rahisi wa kuwafikia watu wengi zaidi na kazi hiyo ilianza jana. | 3 |
Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali, kocha huyo golini atamweka Ally Mustafa, akidhani kuwa ndiye aliyecheza vizuri zaidi katika nafasi hiyo wakati beki wa kulia ni pamoja Juma Abdul wakati mabeki wa katikati ni Paschal Wawa na Nadir Haroub.Mabeki wa kushoto ni Tshabalala kutoka Simba, ambaye alisema hajui jina lake halisi.“Safu ya kiungo ni Said Ndemla kutoka Simba, winga ya kulia ni Msuva, winga wa kushoto Emmanuel Okwi, kiungo cha mbele Niyonzima na washambuliaji wawili ni Amissi Tambwe na Kavumbagu’. “Sikuwepo wakati ligi inaanza, nilianza kazi Yanga mwishoni mwa Desemba mwaka jana, lakini kwa kipindi nilichoona ligi nimewaona wachezaji hao kuwa bora zaidi msimu huu,” alisema kocha huyo raia wa Uholanzi.Kikosi na timu wanazotoka wachezaji hao ni kama ifuatavyo:- Ally Mustafa (Yanga) Juma Abdul (Yanga) Mohamed Hussein ‘Tshabala’ (Simba), Nadir Haroub (Yanga) Paschal Wawa (Azam FC) Said Ndemla (Simba) Simon Msuva (Yanga) Haruna Niyonzima (Yanga) Amiss Tambwe (Yanga) Didier Kavumbagu (Azam FC) Emmanuel Okwi (Simba). | 4 |
ZAINAB IDDY-DAR ES SALAAM WAWAKILISHI wa Tanzania katika mashindano ya Ligi ya
Mabingwa Afrika, Simba, leo watajitupa kwenye Uwanja wa Mazembe mjini
Lubumbashi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na TP Mazembe. Mchezo huo wa marudiano katika hatua ya robo fainali,
unaonekana ni mgumu kwa Simba baada ya kutoka suluhu kwenye Uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam Jumamosi iliyopita. Mshindi wa jumla katika mchezo huo atakutana na
mbabe kati ya Constatine ya Algeria na mabingwa watetezi wa michuano hiyo,
Esperance ya Tunisia katika hatua ya nusu fainali. Kwenye mchezo uliopita Simba ilicheza vizuri mno na
kuihimili TP Mazembe, mabingwa mara nne wa Ligi ya Mabingwa Afrika kiasi cha
kukaribia kushinda mchezo huo ambapo nahodha wake, John Bocco, alikosa penalti. Matokeo haya yameonekana kuwaumiza mashabiki wa
Simba, hasa pale wanapokumbuka rekodi yao ya mwisho walipokutana na Mazembe miaka
nane iliyopita. Mwaka 2011 katika mchezo wa raundi ya kwanza ya Ligi
ya Mabingwa, Simba waliambulia kipigo cha mabao 3-1 mjini Lubumbashi, kabla ya
kuchapwa tena mabao 3-2, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, hivyo kujikuta
wakitolewa kwa jumla ya mabao 6-3, hili pekee linawakatisha tamaa mabingwa hao
wa Tanzania Bara. Simba inahitaji kushinda au kupata sare ya idadi
yoyote ya mabao katika mchezo wa leo ili iweze kusonga mbele. Lakini ukiutupia jicho la tatu mchezo wa Mazembe na
Simba, wawakilishi hao wa Tanzania, bado wana nafasi ya kusonga mbele kutokana
na historia kuonyesha Mazembe wamekuwa wakitolewa mara kwa mara baada ya
kucheza kwao. Rekodi
za Mazembe nyumbani Rekodi mbalimbali zinaonyesha Mazembe wameshindwa
kufanya vizuri katika michezo yao ya nyumbani na kutolewa kwenye mashindano
kadhaa. Historia inaonyesha miamba hiyo ya soka ya Congo tangu
mwaka 1969 hadi hivi sasa hawana rekodi nzuri katika michezo ya kimataifa
wakiwa nyumbani kwani mwaka huo walitolewa na Ismailiy kwa kufungwa mabao 5-3 ambapo mchezo wao wa
kwanza wakiwa Congo walitoka sare ya mabao 2-2 kabla ya kuchapwa mabao 3-1
mchezo wa marudiano. Hali iliendelea kuwa hivyo mwaka 1970 pale
walipoondolewa na Asante Kotoko waliyokutana kwenye fainali na kuchapwa mabao 2-1
kabla ya hapo walishatoka sare ya bao 1-1 wakiwa nyumbani. Mwaka 2013 walipokutana na CS Sfaxiem, waliondolewa
mapema kwenye ligi ya mabingwa baada ya kufungwa mabao 3-2 nyumbani kwao,
lakini pia mwaka 2017 waliondolewa
mapema katika mashindano hayo na CAPS Uniyed ya Zimbabwe, baada ya mchezo wa
kwanza uliochezwa Congo kupata sare ya bao
1-1 kabla ya kuja kutoka sare ya bila kufungana na wenzao kusonga mbele kwa bao
la ugenini. Simba
wakiwa ugenini Pamoja na rekodi za TP Mazembe wakiwa nyumbani,
lakini pia Simba wamekuwa moto pale wanapopambana ugenini. Ukiondoa michezo ya mwaka huu katika hatua za awali,
mwaka 1979 katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, waliwastaajabisha watu
pale walipoichapa Mufulira Wanderers ya Zambia mabao 5-0 wakiwa ugenini. Katika mchezo wao wa kwanza Simba walifungwa mabao 4-0
na kukata tamaa lakini waliwachapa wapinzani wao kwa kuwatandika mabao 5-0
nyumbani kwao mjini Lusaka na hivyo kusonga mbele. Mwaka 2003 baada ya Simba kuichapa BDF XI mabao 4-1,
wakianza kushinda bao 1-0 nyumbani kabla ya ushindi wa mabao 3-1 ugenini katika
mchezo wa awali wa ligi ya mabingwa, walikutana na Santos ya Afrika Kusini
waliwatoa kwa kuwanyuka kwa mikwaju ya penalti 9-8 wakiwa ugenini michezo yote
miwili. Kwenye mchezo wa raundi ya pili Simba ilifanikiwa
kuwatoa mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa, Zamalek ya Misri baada ya
kuwafunga kwa penalti 3-2 kutokana na mchezo wa kwanza Wekundu wa Msimbazi
kufungwa bao 1-0 wakiwa nyumbani kisha nao kwenda kulipiza kwa kuwafunga bao 1-0
ugenini na hivyo kuamuliwa yapingwe matuta. Simba
kusonga mbele inawezekana Kuna msemo wa wahenga unaosema ‘jitihada
hushinda kudra’, hivyo kama Simba wakicheza kwa malengo, nia na kuweka hesabu
zao sawa, basi upo uwezekano wa kupenya hatua ya robo fainali. Hakuna shaka wachezaji na benchi la ufundi
wamejipanga kukabiliana na mikiki mikiki watakayokutana nayo Congo kuanzia
ndani hadi nje ya uwanja. Ndani ya uwanja, wachezaji wanapaswa kucheza
kwa ushirikiano na kila mmoja anatakiwa kutumia nguvu, akili na juhudi binafsi
ili kutimiza majukumu yake kikamilifu. Hii itawasaidia Simba kupata matokeo chanya
kwenye uwanja wa ugenini na kuwapa furaha mashabiki wao ambao wanaiombea timu
yao ipige hatua zaidi kimataifa. Ushindi wa aina yoyote utakuwa na manufaa kwa
Simba, kwani utawawezesha kutinga hatua inayofuata ambayo kila shabiki na
mwanachana wa klabu hiyo anaitamani. Kila kitu kinawezekana chini ya jua, kama
Simba iliwahi kuvunja rekodi na kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa
Afrika mwaka 2013, haitashindwa kufika fainali hii sasa ikiwa ina mahitaji yote
muhimu. | 4 |
Katika mchezo huo ambao ulikuwa mgumu kwa pande zote, Mbeya City ilionekana kuanza vyema baada ya kuhimili dakika 10 za mwanzo ikipeleka mashambulizi mfululizo langoni mwa Yanga.Pamoja na mashambulizi hayo, timu hiyo ilikosa baadhi ya nafasi za wazi, ambapo mshambuliaji Eliud Ambokile alikosa nafasi mbili za wazi huku akigongesha mwamba kunako dakika ya 21.Yanga ilionekana kutulia na kuzima mashambulizi hayo huku ikitumia mipira ya pembeni ambayo mpaka mapumziko haikuwa na madhara kwa wapinzani wao.Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko ya kumtoa Kelvin Yondan aliyeumia tangu kipindi cha kwanza na nafasi yake kuchukuliwa na nahodha Nadir Canavaro.Mpira uliendelea kwa kasi kwa timu zote, lakini Yanga walifanya mabadiliko dakika ya 51 kwa kumpumzisha Emmanuel Martin na kumuingiza Juma Mahadhi.Mabadiliko hayo yalionekana kuwa na tija kwa upande wa timu hiyo ambapo usumbufu wa winga ulifanya mabeki wa Mbeya City kumchezea madhambi na kusababisha adhabu nje kidogo ya eneo la hatari la timu, faulo iliyozaa bao la timu hiyo lililofungwa na kiungo Raphael Daudi dakika ya 57.Dakika ya 60 mchezo huo uliingia taharuki na kusimama kwa dakika kadhaa, baada ya mashabiki wanaodhaniwa kuwa wa Mbeya City kumtupia mawe kipa Youthe Rostand na kufanya mchezo usimame kwa muda.Wakati Yanga ikiendelea kutafuta bao la kujihakikishia ushindi, beki wa Mbeya City, Ramadhani Malima alijikuta akitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Yusuph Mhilu.Baada ya dakika tisini kukamilika mwamuzi Shomary Lawi aliongeza dakika sita kufidia dakika zilizopotea kwa matukio mbalimbali.Pamoja na kuwa pungufu dakika hizo za nyongeza, Mbeya City ilionekana kuwa moto ambapo dakika ya 92 ilisawazisha bao hilo kupitia Idd Selamani akipokea pasi ya Kenny Kunambi.Baada ya matokeo hayo Yanga iliendelea kukaa nafasi ya pili kwa pointi 48 na ikiwa na michezo miwili mkononi. | 4 |
Mwandishi
Wetu Kampuni
ya Agri-Ajira imewapa changamoto ya kujitosa kwenye kilimo cha biashara Kampuni
ya KCL Ltd. kutokana na mafanikio waliyopata ikiwamo kujiajiri. Kampuni
hiyo inayoundwa na vijana wawili, Ibrahim Charles na Samwel Jonathan, imekuwa
chachu kwa Kampuni ya KCL Ltd na vijana wengine nchini kutokana na kuthubutu
kwao na kuwa mfano kwa vijana baada ya kujitosa kwenye kilimo na kulima kwa
mafanikio makubwa ekari 50 za mpunga katika Kata ya Rutinda, Wilaya ya Kilosa, mkoani
Morogoro. Vijana hao kutoka katika kampuni hizo mbili wamekutana leo katika Siku ya Mavuno mkoani Morogoro ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Anthony Mavunde. Licha
ya mafanikio hayo vijana hao wamesema, changamoto zilizopo ni upatikanaji wa
maeneo ya kilimo, uwezeshaji kwa vijana mathalani katika pembejeo na mikopo ya mitaji
ya uwekezaji ambapo wametoa maombi kwa serikali kuwashika mkono vijana ili
waweze kuwa chachu si tu ya kujiajiri ila kuzalisha fursa za ajira kwa vijana
wengine. Kwa
upande wake Mavunde aliahidi kushughulikia changamoto hizo kwa kushirikiana na
Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) kuwawezesha vijana na kuagiza
uongozi wa mkoa na Wilaya ya Kilosa kuhakikisha unatafuta na kutenga maeneo kwa
vijana hao. “Niwasihi
na vijana wengine wajiunge na kilimo na kuhakikisha kilimo kinaleta tija nchini
ili kupunguza umasikini, upatikanaji wa ajira na kuongeza upatikanaji wa
chakula nchini,” amesema Mavunde. Naye
mmoja ya Wakurugenzi wa KCL, Gabriel Munasa, amesema amejifunza mengi ambapo
ameahidi kutumia maarifa aliyopata kwa niaba ya KCL kuhamisha maarifa hayo kwa
kampuni yao ya vijana waliotokana na Group ya WhatsApp na kuwa kampuni katika
kufikia malengo mengi waliyo nayo kama kampuni. | 3 |
Na ASHA BANI
WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) itaanza operesheni ya kuimarisha utekelezaji wa sheria za usafirishaji wa mazao ya misitu hususan mkaa wiki ijayo, kwa lengo la kuwahimiza wananchi wafuate kanuni na sheria hizo.
Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi endelevu ya misitu na nyuki nchini, Mohamed Kilongo, alisema ataongoza timu ya pamoja ya maofisa wa polisi, Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) na TFS, kutekeleza operesheni hiyo endelevu kwenye mikoa yote ya Tanzania Bara kuanzia Aprili 10, mwaka huu.
Alisema lengo ni kuhakikisha ufuataji wa mwongozo wa uvunaji endelevu wa mazao ya misitu, sheria za misitu, sheria ya usalama barabarani na kanuni ya utoaji wa leseni za usafirishaji.
Aliongeza kuwa wamefanya kampeni ya kutoa elimu kwa zaidi ya wiki tatu kuhusu usafirishaji wa mazao ya misitu hususan mkaa, baada ya kubaini kuwa ndicho kichocheo kikubwa cha uharibifu wa mazingira kutokana na kuvunwa kinyume na taratibu kusafirishwa kwa kutumia pikipiki na baiskeli, jambo ambalo ni kinyume na sheria.
Kilongo alisema kulingana na sheria za nchi zilizopo, pikipiki haziruhusiwi kusafirisha mazao ya misitu hususan mkaa, usafirishaji wa mazao ya misitu kwa baiskeli na pikipiki kwani vinakiuka sheria.
Alisema mwongozo wa uvunaji endelevu wa mazao ya misitu wa mwaka 2015, unaeleza kuwa vyombo vya usafiri vinavyoruhusiwa kusafirisha mazao ya misitu ni vile vyenye magurudumu manne.
Aidha, Sumatra chini ya Kanuni ya Transport Licensing (Motor cycle and Tricycles) ya mwaka 2010, inatambua pikipiki kama chombo cha kusafirisha abiria na si vinginevyo. Huku, Sheria ya Usalama Barabarani sura ya 168 iliyorejewa mwaka 2002, inatambua pikipiki na baiskeli kama vyombo vya usafiri kwa ajili ya abiria na si kubeba mizigo.
Aliongeza kuwa kwa tathmini ambayo wamefanya, pikipiki na baiskeli zinachangia uvunaji haramu na usafirishaji wa haraka wa mazao ya misitu hususan mkaa na inakadiriwa kuwa pikipiki 20 zikisafirisha mkaa ni sawa na lori moja la tani 7 lililojaa mkaa.
“Njia hii ya usafiri inahatarisha maisha ya watumiaji wengine wa barabara na wale waoaoendesha vyombo hivyo.. njia hii ya usafiri inachangia ukwepaji wa makusanyo ya maduhuli ya Serikali.
“Sasa kwenye kampeni ambayo tumeifanya ya kuelimisha wanaosafirisha mkaa kwa pikipiki na baiskeli kwa muda wa zaidi ya wiki tatu, ilikuwa ni kuwaelimisha wananchi sheria zinasemaje ambazo zinatuongoza katika maisha ya kila siku sasa kinachofuata ni sheria kutekelezwa,” alisema Kilongo. | 3 |
FORTALEZA, Brazil WENYEJI wa fainali za Kombe la Dunia, Timu ya Taifa ya Brazil, wataingia uwanjani kesho katika mchezo wa robo fainali ya michuano hiyo dhidi ya wababe wa Amerika Kusini, Colombia. Colombia itajitupa kwenye Uwanja wa Estadio Castelao mjini Fortaleza, ikiwa ni baada ya kufanikiwa kuitupa nje Uruguay kwa mabao 2-0 wakati Brazil iliitoa Chile kwa penalti 3-2. Wakati huo huo staa wa Brazil, Neymar ambaye alizua hofu ya kukosa mchezo dhidi ya Colombia amedaiwa kupona majeraha yake hivyo atakuwa miongoni mwa wachezaji watakaocheza kesho. Kwa mujibu wa daktari wa Shirikisho la soka nchini humo (CBF), Jose Luiz Runco alisema kuwa Neymar atakuwa imara kiafya hivyo yupo tayari kwa mchezo dhidi ya Colombia mjini Fortaleza. Kocha wa Brazil, Luiz Felipe Scolari alipata wasiwasi juu ya afya ya nyota wake kutokana na mchezo mbaya aliochezewa na Chile. Baada ya mchezo dhidi ya Chile, Neymar anadaiwa kulalamikia maumivu ya paja la mguu wa kushoto. “Ni maumivu yake ndiyo kitu kinachotuumiza. Atapumzishwa kwenye mazoezi lakini daktari Runco amesema hakuna sababu za kuhofia kwani atamudu kucheza mechi dhidi ya Colombia,” alsiema Rodrigo Paiva msemaji wa CBF. | 4 |
NA ZAINAB IDDY, DAR ES SALAAM WINGA wa timu ya Azam FC, Farid Mussa ambaye yuko katika majaribio nchini Hispania, ameweka wazi kuwa malengo yake ni kucheza katika klabu ya Malaga aliyowahi kuitumikia beki wa Arsenal, Nacho Monreal. Farid alianza majaribio rasmi Hispania Jumatatu iliyopita akiwa na kikosi cha timu ya CD Tenerife inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini humo, kabla ya wiki ijayo kuendelea na majaribo katika timu za Las Palmas na kumalizia Malaga. Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi kutoka Hispania, Farid alisema kuwa licha ya kuwa na uhakika wa kufanya majaribio katika timu hizo tatu, lakini lengo lake ni kupata nafasi ya kuwa moja ya wachezaji katika kikosi cha Malaga. “Wakala wangu John Sorzano raia wa Venezuela, amenihakikishia kufanya majaribio katika timu hizo tatu huku nikianza na CD Tenerife kisha hizo nyingine, lakini binafsi lengo na furaha yangu ni kupata nafasi kwenye kikosi cha Malaga kinachoshiriki Ligi Kuu Hispania ‘La Liga’, ambacho naamini kitanifikisha mbali kisoka. Nyota huyo chipukizi aliyekuzwa na kituo cha kulea vipaji cha Azam FC, atakuwa nchini Hispania kwa takribani wiki tatu na anatarajia kurejea nchini Mei 19 mwaka huu. Iwapo atafuzu katika majaribio hayo, atakuwa Mtanzania wa kwanza kucheza katika klabu kubwa nchini Hispania. | 4 |
WASHINGTON, MAREKANI SIKU chache baada ya Umoja wa Mataifa (UN) kupiga kura kulaani ujenzi wa makazi ya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi na Yerusalem Mashariki, Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, amehoji ufanisi wa chombo hicho, akisema ni ‘genge la watu wakusanyikao na kupiga soga’. Alitoa kauli hiyo baada ya jaribio lake la kutaka kupinga azimio lililokemea mpango wa Israel kuendelea kujenga makazi katika ardhi ya Wapalestina kushindikana. Baraza la Usalama la UN (UNSC) limesema Israel inakiuka sheria za kimataifa kwa kujenga katika ardhi ya Wapelestina. Azimio hilo lilipitishwa Ijumaa iliyopita, huku Trump akitoa onyo kuwa mambo yatakuwa tofauti wakati atakaposhika rasmi hatamu za uongozi wa Marekani. Uamuzi wa utawala wa Rais Barack Obama kujiweka kando wakati UNSC ilipopiga kura hiyo ilihali ina kura ya turufu yenye uwezo wa kuitetea Israel, umekosolewa na Trump na kulaaniwa vikali na Israel. Awali Desemba mwaka jana, Trump aliwahi kukaririwa akisema angependa kutoegemea upande wowote katika masuala ya Israel na Palestina. Lakini msimamo wake ukawa ukibadilika kadiri kampeni za urais zilipoendelea akiegemea Israel zaidi. Licha ya shutuma za Trump kwa UN, chombo hicho kwa miaka mingi kinashutumiwa na baadhi ya Serikali za magharibi kukosa ufanisi, huku mataifa yanayoendelea yakisema kinaburuzwa na mataifa tajiri. | 2 |
KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema kutokuwa na uzoefu wa kutosha kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ni chanzo cha kupoteza mchezo wa marudiano wa robo fainali dhidi ya TP Mazembe ya DR Congo.Mchezo huo wa marudiano ulipigwa mjini Lubumbashi ambapo Simba walipoteza mechi hiyo ya ugenini kwa kufungwa mabao 4-1 na kutolewa kwenye michuano hiyo baada ya kutoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.Rekodi ya kupoteza michezo ya ugenini kwa mabao mengi imeonekana kuisumbua Simba kwenye michuano hii ambapo kwenye kampeni zake ilishinda mechi moja tu ugenini dhidi ya Mbabane Swallows ya eSwatini.Aussems alisema mechi hiyo ilikuwa ngumu kwao kwa kuwa wapinzani wao wana uzoefu hasa kwenye michezo ya hatua hiyo na kwamba wametolewa na wanajipanga wakiamini msimu ujao watakuwa na uzoefu baada ya kuona changamoto.“Mchezo tulianza vizuri tulipata bao la mapema lakini wachezaji wangu walishindwa kulinda ushindi kutokana na wapinzani wetu kucheza kwa kumiliki mpira wakati wote hasa sehemu ya kiungo na kupata ushindi walioupata,” amesema Aussems.Alisema kwa sasa nguvu zao wanaelekeza kwenye Ligi Kuu Bara kuhakikisha wanashinda mechi zilizobaki ili kutetea taji hilo na mwakani wapate tena tiketi ya kushiriki michuano hiyo.“Saa hizi nguvu tunahamishia kwenye michezo ya ligi, tunajua tuna ratiba ngumu kwa kuwa tuna michezo 16 kutokana na ratiba yetu kuwa ngumu lakini tutajitahidi kila namna kupata ushindi utakaotuweka vizuri kwenye kutetea ubingwa wetu,” alisema. | 4 |
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya, alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele. “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema | 5 |
Hayo yamo kwenye taarifa iliyotolewa jana wakati benki hiyo ikisherehekea miaka mitatu ya utoaji wa huduma kwa wateja.Akizungumza na Wakurugenzi wa Bodi, Wafanyakazi na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kusherehekea mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Covenant Bank, Sabetha Mwambenja alisema wamepata mafanikio makubwa katika kipindi kifupi kutokana na aina ya huduma wanazotoa.Alisema hiyo ni zaidi na matarajio ya Benki Kuu ambayo iliamini benki hiyo itaanza kutengeneza faidi kuanzia miaka mitatu.Alisema kuanzia Juni mwaka jana, hadi Juni mwaka huu, pato la benki limeongezeka kutoka Sh milioni 951 hadi kufikia Sh bilioni 2.9. Faida imepanda kutoka Sh milioni tano hadi Sh bilioni 1.4. Amana ilikuwa Sh bilioni 10.2 na imefikia Sh bilioni 13.4.“Fedha za wahisani zimeongezeka kufikia Sh bilioni 2.23 licha ya mtaji huo kutumika katika uanzishaji wa benki na hasara ya Sh milioni 500 iliyopatikana katika mwaka wa kwanza wa huduma,” alisema Mwambenja.Alisema mafanikio hayo yametokana na ubora wa huduma ambazo zimebuniwa na kuwa benki ya kwanza kutoa aina ya huduma za kipekee kwa kulenga Watanzania ambao wako katika sekta zisizo rasmi.Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Balozi Salome Sijaona, amempongeza Mkurugenzi na Wafanyakazi wa benki hiyo kwa kufanya kazi bila kuchoka. Alisema bodi inatambua mchango wa wafanyakazi hao na kuendelea kuboresha masilahi yao, huku akisisitiza kuwa benki itaendelea kulenga Watanzania wasio katika sekta rasmi. | 5 |
Na NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM SERIKALI imelizuia Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu (Human Rights Watch) kuzindua ripoti inayoelezea namna wafanyakazi wa ndani wa kitanzania wanavyonyanyaswa katika nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Utafiti huo ulifanywa na shirika hilo hapa nchini kwa kuwahoji wasichana kadhaa waliowahi kufanya kazi nchi za UAE na jana ripoti hiyo ilitarajiwa kuzinduliwa. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Ofisa kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. William Kindeketa, alisema watafiti hao hawakufuata taratibu zinazotakiwa na wala hawakuwa na kibali cha kufanya utafiti huo. “Tulivyomuhoji huyu mtafiti tumebaini alikuwa hajapitia taratibu zinazotakiwa, hana viza ya utafiti wala kitu chochote, ndio maana tulimwambia hili ni kosa,” alisema Dk. Kindeketa. Alisema kabla ya kufanya utafiti, mtu au shirika anatakiwa aandike dokezo na kuliwasilisha Costech kwa ajili ya kupitiwa na kamati maalumu inayohusika na masuala ya utafiti na kama likikidhi vigezo muhusika hupewa kibali cha kuendelea na utafiti wake. “Katika nchi yoyote ukitaka kufanya utafiti lazima ufuate utaratibu, hata hapa kwetu tuna utaratibu huo. Uwe utafiti wa kijamii, sayansi au wowote ule Costech ndio wenye mamlaka. “Unatakiwa uandike dokezo lako kisha unaliwasilisha Costech, wataalamu wataliangalia halafu litapelekwa kwenye kamati ya taifa ya kusajili tafiti, wao wanaweza kulikataa ama kulikubali. “Na kama si Mtanzania ukishapata kibali lazima uende uhamiaji kupata kibali cha ukaazi. Utafiti huu umefanyika hapa kwa kuhoji wafanyakazi ambao walisharudi kutoka Oman lakini wahusika hawakufuata utaratibu na hili ni somo katika taasisi zingine,” alisema. Naye Mtafiti wa Human Rights Watch katika nchi za Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika, Rothna Begum, alisema walifuata taratibu lakini wameshangaa kuzuiliwa kuzindua ripoti hiyo. “Leo (jana) asubuhi kuna maafisa kutoka Costech wamekuja na kutuambia kwamba hatukufuata taratibu za kufanya utafiti huu hivyo, haturuhusiwi kuizindua ripoti yetu. “Tumefuata taratibu zote ambazo huwa zinatakiwa kabla ya kufanya utafiti na tulikuwa na mikutano na wizara tofauti kabla ya kuja hapa kutaka kuizindua ripoti hii. “Tumekuja mara nyingi Tanzania kuzindua ripoti lakini kwa hii ya leo (jana) wamesema kwamba kuna taratibu ambazo hatujazifuata. “Huwa tunaandika barua kwa serikali na kuwaambia kuhusu utafiti tunaotaka kuufanya na tulizungumza nao na mazungumzo yalikuwa mazuri hadi sasa,” alisema Begum. ILIVYOKUWA Uzinduzi wa ripoti hiyo ulipangwa kufanyika katika Hoteli ya Holday Inn, Dar es Salaam na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari walialikwa kuhudhuria. Waandishi walipofika waligawiwa nakala za ripoti hiyo lakini kabla ya kuanza kwa mkutano huo, ghafla walifika maofisa wawili wa serikali Dk. Kindeketa na mwingine aliyetambulika kama Ally Kapola na kulizuia shirika hilo lisiendelee na uzinduzi huo. Hali hiyo ilisababisha maafisa wa shirika hilo kutoka nje ya ukumbi kwenda kujadiliana na maofisa hao wa serikali huku waandishi wakiendelea kusubiri. Majadiliano hayo yaliyodumu kwa dakika kadhaa hayakufua dafu kwani maofisa wa shirika hilo na waandishi wa habari waliamriwa waondoke eneo hilo. | 3 |
WAKAZI watatu wa kijiji cha Pangawe, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro wanashikiliwa na Polisi kutokana na tuhuma za kukutwa wakiuza nyama ya ng’ombe waliokufa na kufukiwa baada ya kubainika kuwa na ugonjwa wa kimeta.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa alisema jana mjini hapa kuwa, tukio hilo lilitokea Mei 18, mwaka huu saa 2: 30 asubuhi katika kijiji cha Pangawe, Kata ya Mkambarani, Wilaya na Mkoa wa Morogoro.Kamanda Mutafungwa alisema ng’ombe hao saba walikufa na kufukiwa baada ya kubainika kuwa na ugonjwa wa kimeta baada ya kuthibitishwa na daktari wa mifugo wa halmashauri hiyo, Dk Annastazia Julian.Kwa mujibu wa Kamanda huyo, ng’ombe hao walikuwa wanamilikiwa na mfugaji Dickson Msurwa, mkazi wa Nanenane, Manispaa ya Morogoro anayefugia mifugo yake katika kijiji cha Pangawe.Alisema mizoga hiyo ya ng’ombe ilifukuliwa na Salumu Ramadhani ambaye alikamatwa akiwa na mapaja mawili nyumbani kwake pamoja na wenzake ambao walisadikiwa kwenda kuuzwa katika eneo la Kingolwira na maeneo mengine.Alisema baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Pangawe, Matata Ndida, msako mkali ulianza wa kuwatafuta watuhumiwa na ndipo walipoweza kukamatwa.Kamanda Mutafungwa aliwataja wengine waliokamatwa kuwa ni Salumu Ramadhani, Matata Shija na Joseph Mhangama ambao ni wakazi wa kijiji cha cha Pangawe, kata ya Mkambarani, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.Alisema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara baada ya taratibu kukamilika ili kujibu mashitaka yanayowakabili. | 3 |
SERIKALI imeanzisha kanzidata ya kuorodhesha wataalamu wa Kiswahili kwa lengo la kuwatumia kufundisha lugha hiyo kwa wageni na mataifa mbalimbali ulimwenguni.Akifunga mafunzo ya wiki moja ya walimu wa kufundisha Kiswahili kwa wageni, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema hivi sasa kanzidata hiyo iliyoanzishwa na wizara hiyo ina wataalamu wa kufundisha Kiswahili kwa wageni na nje ya nchi 380.Alisema baada ya wataalamu hao kupatikana sasa, atakaa na waziri wa elimu, sayansi na teknolojia na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kuelezea uwepo wa wataalamu wao kwa lengo la kutangaza popote fursa za kufundisha lugha hiyo zinapopatikana.Amesema Watanzania wanatakiwa kutumia fursa ya kujua Kiswahili ambacho ni miongoni mwa lugha 10 kubwa duniani ili kuhakikisha wanaitangaza nchi na kwa kufundisha somo hilo.Dk Mwakyembe alisema wahitimu hao ambao wameivishwa, watatumika kufundisha wageni Kiswahili na kufundisha lugha hiyo katika nchi mbalimbali duniani.Alisema vyuo vikuu vyote nchini na redio kubwa duniani, zinatumia Kiswahili, hivyo Watanzania wajue kwamba wanayo fursa za kutangaza Kiswahili popote duniani wanachotakiwa ni kujiamini.Amesema Kiswahili kilianza kutambuliwa tangu wakati wa Uhuru wakati ambao Mwalimu Julius Nyerere, aliamua kuunda Wizara ya Utamaduni na Vijana kwa lengo la Watanzania kudumisha utamaduni wao kwa kutumia lugha yao.Akizungumza Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Tanzania, Consolata Mushi amesema baraza hilo limejiandaa katika kuandaa wataalamu wa kufundisha lugha kwa wageni nchini.Alisema mafunzo ya Kiswahili kwa wageni ni muhimu na hivyo wataalamu hao, wataongeza idadi ya wataalamu wa lugha katika kanzidata ya wizara ambayo ipo rasmi kwa ajili ya kuwatangaza.Akisoma risala ya wahitimu, Neema Mkobalo alisema wahitimu wa mafunzo hayo 68, wapo tayari kulitumikia taifa kukitangaza Kiswahili kwa kuwafundisha wageni.Amesema mafunzo hayo ya wiki moja, yamewajengea uwezo kutokana na utaalamu wa walimu wao kutoka Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) na Bakita na hivyo wameiva kwa kufundisha wageni Kiswahili.Amemwomba Waziri Mwakyembe awasaidie kuomba ruhusa kwa waajiri wao mbalimbali kwa kuwapa kibali cha kusoma, kutokana na waajiri wengi kuwakataliwa kupata ruhusa hiyo. | 3 |
NA ZAINAB IDDY-DAR ES SALAAM SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (FIFA), limepitisha panga kwa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), baada ya kulitaka kupunguza idadi ya wajumbe wake kutoka 23 hadi 13. Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau, alisema wamepokea mapendekezo kutoka FIFA yanayowataka kufanya mabadiliko ya katiba ya shirikisho hilo. “Kulingana na mapendekezo hayo, mambo ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho ni idadi ya watu katika Kamati ya Utendaji na kipindi cha kufanya mikutanao.. “Kwa mujibu wa Fifa, Kamati ya Utendaji inatakiwa kuwa na watu 13 kutoka 23, lakini pia kuwa na vikao kila baada ya miezi miwili na si miezi mitatu. “TFF imeangalia mapendekezo hayo pamoja na uhitaji wa watu katika Kamati ya Utendaji na kupeleka mapendekezo mengine ambayo tunaona yatatusaidia katika utendaji kazi wetu, kwani idadi iliyotakiwa kupungua ni asilimia 45. “Wajumbe wa mkutano mkuu wanatakiwa kupungua kutoka 129 hadi 87, ikimaanisha katika mikoa 26 kila mmoja utatoa wajumbe wawili, wakati 20 watatoka kwenye klabu na vyama vitatoa wajumbe 15 tu,” alisema Kidau. Februali mwaka jana, Rais wa Fifa, Gianni Infantino alishiriki mkutano mkuu wa shirikisho hilo uliofanyika hapa nchini. Ni wazi agizo hilo la Fifa linalengo la kupunguza gharama za uendeshaji wa taasisi hiyo inayosimamia mchezo wa soka hapa nchini. Katika hatua nyingine, Kidau alisema mabadiliko ya Katiba ya TFF yaliyofanyika katika mkutano mkuu jijini Arusha, yaligusa moja kwa moja mfumo wa uongozi kuelekea uchaguzi ujao. “Moja ya sehemu iliyoguswa katika marekebisho ya katiba ni nafasi ya makamu wa rais, ambayo itakuwa ni ya kuteuliwa na rais atakayechaguliwa badala ya kuchaguliwa kama ilivyo sasa,”alisema Kidau alisema mkutano mkuu wa kawaida wa shirikisho hilo umepangwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar es Salaam, hivyo upo uwezekano wa kujadili mapendekezo yaliyotolewa na FIFA. Wakati huo huo, Kidau alisema aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Tanzania(TPLB), Boniface Wambura ameteuliwa kuwa Mkuu wa Idara ya Habari na Masoko ya TFF. Alisema amepewa kitengo hicho, baada ya kumaliza mkataba wake TPLB mwanzoni mwa mwezi huu. “Wambura ni mzoefu katika masuala ya habari kitaaluma na kwa kuwa TFF ina mpango wa kutanua idara ya habari na masoko kwa kuanzisha online radio, magazine na kuboresha ‘newsletter’ Kamati ya Utendaji imeona ni mtu sahihi kukaa hapo. “Kwa maana hiyo, siku si nyingi tutatoa tangazo la ajira katika nafasi ya Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi| na tunatarajia kumpata mtu bora,” alisema Kidau. Kidau pia alisema Kamati ya Utendaji ya TFF, imemteua Oscar Milambo kuwa Mkurugenzi wa Ufundi. Mirambo anachukua nafasi ya Ammy Minje, aliyemaliza muda wake, huku akitarajiwa kushiriki mafunzo ya uongozi yanayotolewa na Fifa. | 4 |
Na Waanidishi Wetu,
SUALA la uhakiki wa vyeti feki limezidi kuitikisa sekta ya afya ambapo maelfu ya watumishi wamejikuta wakipoteza kazi na zahanati na vituo vya afya vikifungwa.
Hatua hiyo inatokana na ripoti ya uhakiki wa watumishi wa umma nchini iliyokabidhiwa hivi karibuni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki kwa Rais Dk. John Magufuli mjini Dodoma.
Katika sekeseke hilo watumishi 18 wa idara ya afya katika hospitali ya rufaa Bombo wamejikuta wakipoteza kazi kutokana na hali hiyo.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk. Goodluck Mbwilo, alisema kuwa idara ya wauguzi ndiyo iliyoathirika zaidi.
“Eneo ambalo limeathirika zaidi ni idara ya uuguzi na kutokana na hilo wauguzi 13 wamebainika kuwa na vyeti feki, matabibu wawili na madereva watatu,” alisema Dk. Mbwilo
Kiteto
Watumishi 65 wamebainika kuwa na vyeti feki wilayani Kiteto mkoani Manyara.
Maeneo yaliyoathirika zaidi ni sekta ya elimu na afya ambazo zinaongoza kwa watumishi wake kuathiriwa na hali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Tamimu Kambona, akizungumza na MTANZANIA amekiri kuathiriwa na zoezi hilo na kudai ongezeko la uhaba wa watumishi linazidi kukua.
Muleba
Uhakiki huo wa watumishio wenye vyeti vya kughushi umezidi kuathiri wananchi katika upatikanaji wa huduma za jamii katika Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, wameondolewa watumishi 53 kati yao 22 wanatoka idara ta afya.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Dk Modest Lwakahemula, alisema hayo katika kikao cha Baraza la Madiwani ambako alisema kwenye baadhi ya zahanati na vituo vya afya wananchi wanakosa huduma kutokana na hali hiyo.
Arusha
Watumishi 503 wa umma wakiwamo wa idara ya afya na elimu, wamebainika kuwa na vyeti vya kughushi.
Rungu hilo pia limemwangukia mwanasheria wa Halmashauri ya Arusha, DC, wakunga, walimu, madereva na wahudumu wa ofisi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega, aliiambia MTANZANIA jana kuwa uhakiki huo ulifanywa kwa watumishi 15,777 huku sekta zilizoathiriwa zaidi ni afya, elimu na utawala.
Habari hii imeandaliwa na Amina Omari (Tanga), Abraham Gwandu (Arusha), MOHAMED HAMAD (Kiteto) na KAHINDE KAMUGISHA (Muleba). | 0 |
KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema walicheza vibaya kwenye mechi yao na Kagera Sugar na ndio sababu ya kufungwa.Amesema pamoja na matokeo mabaya waliyoyapata ya kufungwa mabao 2-1 na Kagera Sugar, wameshasahau na sasa wanajipanga kuikabili Alliance kesho.Kagera Sugar ilimaliza ushindi wa mechi 11 mfululizo wa Simba na kufunga kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba juzi.Simba jana iliwasili jijini Mwanza tayari kwa mechi hiyo ya kesho itakayochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.Akizungumza baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, Aussems amesema yaliyotokea Bukoba yameshapita sasa ni zamu ya kupambana na kutimiza lengo lao la kutetea ubingwa.Amesema katika mpira kuna wakati wa kushinda, kupata sare na kufungwa lakini yote ni sehemu ya matokeo.Aussems amesema japo ratiba si rafiki kwao kwani wanatakiwa kucheza kila baada ya siku mbili, lakini watajipanga kushinda mechi zao.Simba imekuwa na ratiba ngumu ya viporo kutokana na kushiriki michuano ya kimataifa ambapo iliishia robo fainali za Ligi ya Mabingwa Afrika.Kocha huyo wa zamani wa timu za KSA Cameroun, Stade de Reims na Nepal alisema timu yake imekuja na wachezaji 24 hivyo atakuwa akifanya mabadiliko katika kikosi chake ili kupata matokeo katika michezo yao iliyobakia.Beki huyo wa zamani wa timu ya E.S Troyes alisema wachezaji wake wote wapo tayari kwa ajili ya michezo yao ya kanda ya Ziwa.Ikimaliza mechi ya kesho, Simba itasafiri mpaka Mara kucheza na Biashara ya huko kabla ya kurudi Dar es Salaam kucheza na KMC.Katika msimamo wa Ligi Kuu, Simba ipo katika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 60 baada ya kucheza michezo 24.Mabingwa hao watetezi wameshinda mechi 19, sare 3 na imepoteza michezo minne ikifunga mabao 51 na kufungwa mabao 10. | 4 |
RAIS John Magufuli amekonga nyoyo za Watanzania kwa uamuzi wake wa kutekeleza mradi wa kufua umeme wa maji wa Rufiji.Juzi Ijumaa, Rais Magufuli aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo mkubwa wa kufua umeme utakaozalisha megawati 2,115. Mradi huo unatekelezwa katika Pori la Akiba la Selous wilayani Rufiji mkoani Pwani na mkandarasi wake ni kampuni za ubia za Arab Contractors na Elsewedy zote za Misri.Baadhi ya wananchi na viongozi waliohudhuria uzinduzi huo wamempongeza Rais Magufuli kwa hotuba nzuri iliyoonesha jinsi anavyojali maisha ya Watanzania bila kutishwa na kelele za wasiotakia mema Tanzania.Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Morogoro, Vitalis Lipagila alisema uamuzi wa Rais Magufuli kutekeleza mradi wa Rufiji ni wa uthubutu mkubwa.“Kama alivyosema mwenyewe kelele nyingi zilipigwa juu ya mradi huu. Kwa kweli Rais wetu ni mtu wa kuthubutu na asiyeyumba,” alisema Lipagila na kuongeza kuwa CCM Mkoa wa Morogoro inamuunga mkono na itasimama naye kidete katika kufanikisha mradi huo.Mkazi wa Kisaki mkoani Morogoro, Jabir Shikamkono alisema taifa linajivunia kutekelezwa kwa mradi huo wenye manufaa makubwa.Shikamkono alisema mradi huo licha ya kuwa wa manufaa kitaifa, lakini pia wao watafaidika moja kwa moja kwani wako jirani na mradi huo utakaokamilika Juni mwaka 2022.“Kwa kweli Rais amekonga nyoyo za watu. Mradi huo manufaa yake yatakuwa makubwa kwa taifa. Tumefurahi sana na tunaamini ukombozi unakuja,” alisema.Mkazi wa Mloka wilayani Rufiji, Pili Mtandika alisema Rais Magufuli amewafurahisha sana kwa sababu awali walijiona kama wametengwa. “Kwa kweli Rais tunamuombea aendelee na wema huu. Tunamtakia heri na fanaka kwa sababu mwanzo tulijiona tumetengwa,” alisema Mtandika. Mwajuma Saleh anayeishi Kisaki alisema wamefarijika na hotuba ya Rais Magufuli na hasa alipotamka kuwa wananchi wa maeneo ya jirani na mradi wapewe kipaumbele.“Nimefurahi Rais kusema wananchi wa maeneo ya jirani wapewe kipaumbele. Naamini sisi vijana tutapata nafasi ya kushiriki katika mradi,” alisema Saleh.Akitoa dua kabla ya kuanza kwa shughuli hiyo, Katibu wa Bakwata Wilaya ya Rufiji, Thabit Mbonde alimpongeza Rais Magufuli kwa kusimama kidete na serikali yake kuwaletea wananchi maendeleo.“Nampongeza Rais Magufuli kwa ujasiri wa kutekeleza miradi ya maendeleo licha ya mikikimikiki unayokumbana nayo. Kaza buti. Hapa Kazi Tu,” alisema Mbonde na kushangiliwa na waliohudhuria hafla hiyo.Mchungaji Godfrey alisema Rais Magufuli anafanya kazi ngumu na nzito na kuwaomba watanzania waendelee kuunga mkono na kumuombeaAkizungumzia hotuba hiyo ya Rais Magufuli, Kaimu Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Leila Muhaji alimpongeza Rais kwa hotuba nzuri na kwamba Tanesco watatekeleza yote aliyoyaagiza. Lakini Leila aliwahimiza wananchi wa maeneo ya jirani na mradi kuchangamkia fursa kama alivyoeleza Rais Magufuli.“Hili la kuchangamkia fursa ni jambo zuri sana. Kama alivyoeleza Rais, zipo fursa nyingi wakati huu wa ujenzi. Tanesco tunawahimiza wananchi wajitokeze kuweza kupata nafasi ya kutoa mchango wao katika mradi wao,” alisema Leila.Katika hotuba yake, Rais Magufuli alisema Tanzania ni Taifa huru na sio nchi masikini, hasa ilipoamua kutekeleza mradi huo wa megawati 2,115.Alisema kelele zinazopigwa kuhusu mradi huo ni kwa sababu wapo watu wenye maslahi binafsi wanaoumia kwa Tanzania kutekeleza mradi huo na kuwa Tanzania imeudhihirishia ulimwengu kuwa unapoamua kutekeleza miradi yako usihangaike kutafuta maoni ya watu wengine kwani wapo watakaokuwamisha.Aidha, alisema ametimiza ndoto za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliyeasisi wazo wa kuwa na mradi wa kufua umeme katika Bonde la mto Rufiji.Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais Magufuli kuhutubia Taifa, Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani alisema Rais Magufuli ametimiza ndoto mbili za Mwalimu Nyerere. Dk Kalemani alizitaja ndoto hizo kuwa ni kuhamia Dodoma kwa Makao Makuu ya nchi na sasa mradi wa kufua umeme wa maji | 3 |
Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM
KUZIBA kwa mishipa ya damu kumetajwa kuwa chanzo kikuu kinachosababisha vifo vingi vya ghafla ambavyo mara nyingi hutokea mtu akiwa usingizini.
Akizungumza na MTANZANIA Jumapili juzi, daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dk. Pedro Pallangyo, alisema tatizo hilo linazidi kuongezeka hasa katika nchi zinazoendelea.
“Mshipa wa damu ukiziba husababisha mtu kupata mshtuko wa moyo na inapotokea hali hiyo mtu akiwa usingizini, hufariki dunia,” alisema.
Alisema zipo sababu hatarishi nyingi zinazochangia kuziba kwa mishipa ya damu, ikiwamo ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, unywaji pombe kupita kiasi, uvutaji sigara, uzito mkubwa na kutokufanya mazoezi.
“Hizi ni sababu ambazo mtu anao uwezo wa kuziepuka, lakini zipo sababu nyingi kwa mfano ugonjwa wa kisukari au shinikizo la damu wakati mwingine huwa yanarithiwa,” alisema.
Dk. Pallangyo alisema kiwango cha mafuta kikiwa kikubwa katika damu kuliko inavyotakiwa, huenda kuziba mishipa ya damu na kwamba athari huanza kuonekana mtu anapofikisha umri wa miaka 40 hadi 45.
“Lakini kadiri miaka inavyokwenda mbele, tatizo linazidi kujitokeza zaidi katika kundi la vijana, hapa JKCI kwa siku tunachunguza kati ya watu watatu hadi watano kujua kama wana tatizo hili.
“Kwa wiki tunaona wagonjwa wapatao 35 ambao ukikadiria kwa mwezi ni kati ya wagonjwa 140. Mwaka 2015/16 tuliwachunguza takribani watu 400 katika mtambo wetu maalumu wa ‘cath lab’,” alisema.
Daktari huyo alisema asilimia 45 kati ya watu hao waliochunguzwa afya zao, walikutwa mishipa yao imeziba na hivyo kuhitaji kufanyiwa upasuaji. | 3 |
NA JOHANES RESPICHIUS MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Juma Musa ‘Jux’, amesema alianza kupata umaarufu kabla ya mpenzi wake, Vanessa Mdee, hivyo si sahihi kudai kwamba anatembelea nyota ya mrembo huyo kwenye sanaa ya muziki. Akizungumza na MTANZANIA, Jux alisema kama alikuwa anataka kufahamika kupitia Vanessa wangeshafanya wimbo wa kushirikiana kwa kuwa ni wapenzi kwa sasa. “Nilianza kufanya muziki na kupata umaarufu kabla ya Vannesa, hivyo mimi nilianza kuwa staa kabla yake ila yeye anaonekana staa kwa kuwa anajituma zaidi ya wasichana wengine na pia anafanya muziki mzuri kuliko wasichana wengine na nafasi yake ya ushindani na wasanii wenzake ni ndogo hivyo yeye anaonekana zaidi kuliko wengine, uhusiano wetu usitumiwe kupotosha hilo na ndiyo maana kwenye maonyesho au mahojiano ni vigumu kutuona pamoja,” alisema Jux. Jux aliongeza kuwa anavutiwa na Vanessa kwa sababu anajituma na anampa changamoto ya kutafuta mafanikio kila siku ndiyo maana Vanessa ni mwanamke bora kwake. “Mimi napenda changamoto kwa kuwa napenda kuwa tajiri ndiyo maana najiwekeza sana katika biashara mbalimbali ili nitimize ndoto zangu na suala la mtoto bado miaka minne hivi,” anaeleza Jux mwenye miaka 26. | 1 |
NORA DAMIAN Na LEONARD MANG’OA-DAR ES SALAAM MAGWIJI wa siasa wamejitokeza kumzika mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, huku wakimsifu kuwa alikuwa mtu mashuhuri. Kingunge aliyefariki dunia Februari 2, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akitibiwa, baada ya kushambuliwa na mbwa wake Desemba 22, mwaka jana, alizikwa jana katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya viongozi walimwelezea Kingunge kama mtu muhimu nchini, ambaye hajapata kutokea. Akitoa salamu za Serikali, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo, alisema Kingunge ni miongoni mwa watu waliotoa mchango mkubwa uliosababisha nchi kupata heshima. “Kingunge ameacha historia kubwa katika nyaraka mbalimbali za Serikali, ni miongoni mwa watu waliotoa mchango mkubwa nchini hadi tukapata heshima kubwa. “Waliopewa dhamana katika nafasi mbalimbali tujifunze kuweka mbele uzalendo ili kumuenzi Kingunge,” alisema Jafo. BARAZA LA VYAMA Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, John Shibuda, alisema Kingunge alikuwa shujaa wa vitendo vilivyo sanifu na aliyejenga mwelekeo hai wa siasa za Tanzania na ukombozi wa Bara la Afrika. “Ametuachia ufadhili wa maono na uzalendo, alikuwa shujaa wa kuishi, na imani zake za uzalendo hazikubinuliwa na imani yoyote ile,” alisema Shibuda. WASIRA Aliyekuwa waziri katika Serikali za awamu nne, Stephen Wasira, alisema Kingunge alikuwa mjenzi wa hoja, aliyeamini hoja zinajibiwa kwa hoja. “Nilipokuwa Waziri wa Serikali za Mitaa mwaka 1987, nilibahatika kufanya kazi na Kingunge nikiwa chini yake, wakati huo alikuwa na ofisi mbili, Dar es Salaam na Dodoma. “Aliamini katika nguvu ya hoja na si hoja ya nguvu, hivyo pale ulikuwa humwelewi alijitahidi kujenga hoja. “Ni mwanaharakati, lakini ni mshiriki mkubwa katika ujenzi wa Tanzania, tunasikitika kumkosa, lakini hatuna cha kufanya, tunamshukuru Mungu kwa yote,” alisema Wasira. MEMBE Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, alisema ushindi wote ambao CCM imekuwa ikiupata katika chaguzi mbalimbali, kwa kiasi kikubwa ulichangiwa na mwanasiasa huyo. “Ametuachia vitabu vingi sana, kila ukiangalia ilani za uchaguzi, ilani za chama, miongozo ya CCM, kwa sababu alikuwa mjumbe wa Kamati Kuu na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, karibu miaka yote anatoa ushauri. “Yeye ndiye alikuwa anaandika na kuasisi ilani za CCM na ushindi wote uliokuwa unapatikana, alijikita katika masuala ya siasa, hivyo kwa sisi watu wa Mkoa wa Lindi, tumepoteza lulu ambayo ilikuwa inatoa ushauri kwa vijana wote, hasa walioingia katika medani ya siasa. Yeye ndiye alikuwa kungwi wetu na hakujali anamshauri nani,” alisema Membe. Alisema ili kumuenzi, ni vema kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kutokuoneana, kuzushiana kwa sababu Kingunge alikuwa mkweli na alitekeleza kile alichokiamini. “Itatuchukua muda kupata shoka la aina hii, ambalo linaacha kila kitu kwa ajili ya kulitumikia taifa ndani ya chama na ndani ya Serikali. “Alichotuachia katika miaka 41 ya CCM, ni kujenga demokrasia ndani ya Serikali na ndani ya chama, ukitaka kwenda kinyume na mzee Kingunge, kataa suala la demokrasia, hawezi kuwa rafiki yako,” alisema. MANGULA Makamu Mwenyekiti wa CCM – Bara, Philip Mangula, alisema Kinguge aliamini katika nguvu ya hoja na si kwa kulazimisha. “Kingunge alishawishi, hivyo viongozi wote tuige mfano huu wa kushawishi badala ya kulazimisha,” alisema Mangula. NAPE Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye (CCM), alisema Kingunge alikuwa na msimamo, uwezo wa kuthubutu na uzalendo, hivyo ni vema wanasiasa vijana wakaiga mfano huo. “Jambo kubwa la kujifunza kwa Kingunge ni kuwa na msimamo na kutoogopa kutofautiana na wenzako, hata kama ni wakubwa namna gani, hasa pale ambapo wanafanya jambo ambalo huliamini,” alisema Nape. MAALIM SEIF Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, alisema: “Ni vizuri kuyaenzi yale aliyoyasimamia mzee wetu, alikuwa anachukia uonevu dhidi ya mtu na mtu.” MBOWE Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, alisema kwa muda mfupi waliofanya naye kazi, waligundua kuwa alikuwa kiongozi mwenye ushauri mwema, mwenye kupenda kujenga mshikamano. “Ni kiongozi ambaye kile anachokiamini alikuwa akikipigania bila kujali atapoteza nini upande wa pili, aliheshimu sana muda, kama mlikuwa na ahadi mkutane saa 9, atafika muda huo, ni kiongozi wa tofauti sana. “Tunaomba viongozi wa vyama vyote tuige kwa viongozi kama hawa, ambao ni nadra sana katika taifa kuwa nao, hawana chuki, hawana visasi kwa watu, wanapenda kusikiliza mawazo ya wadogo, wakubwa, lakini wana misimamo ya kuleta umoja na mshikamano na si kulitawanya taifa na kutengeneza madaraja ya viongozi,” alisema Mbowe. SOPHIA SIMBA Mwenyekiti wa zamani wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), Sophia Simba, alisema itachukua muda kumpata mwanasiasa kama Kingunge ambaye hakuwa mnafiki. “Ni gwiji la siasa, alijitambua na huwa haropoki, alikuwa akitumia kichwa chake, ameondoka na yale ambayo itatuchukua muda kumpata mwanasiasa kama yeye,” alisema. JENERALI ULIMWENGU Mwandishi wa habari mkongwe, Jenerali Ulimwengu, alisema Kingunge alikuwa na uwezo mkubwa wa kuchambua masuala na kuyaeleza kwa lugha fasaha inayoeleweka na kila mtu. “Alikuwa na fikra pevu, alisoma na akajifunza kuwa mchambuzi wa masuala ya kifalsafa, kisiasa na uongozi wa jamii. “Alikuwa haogopi kutoa msimamo wake kama unawafurahisha ama hauwafurahishi wakubwa, alieleza misimamo yake hata kama Mwalimu Nyerere hakuifurahia, na mwaka 1978 aliwahi kufukuzwa katika jengo la Karimjee akiwa yuko ndani ya Serikali. Tumuenzi kwa kuwa wakweli, kupunguza unafiki na woga,” alisema Ulimwengu. LEMBELI Aliyekuwa Mbunge wa Kahama Vijijini, James Lembeli, alisema ni vigumu kumwelezea Kingunge kwa sababu aliyaishi maneno yake. “Vitendo vyake viliendana na maneno yake, sidhani kama kuna kiongozi mwingine ukiacha Mwalimu Julius Nyerere. Mwalimu alikufa masikini na huyu mzee nadhani amekufa masikini. “Hakuwa na visasi wala kinyongo, hata kwa wale waliomtukana, waliombeza na ndiyo maana amezikwa na umati mkubwa wa watu. “Watu wa vyama vyote wamekuja, viongozi tuliobaki tutumie historia kuturejesha kwenye mstari,” alisema Lembeli. VIONGOZI WENGINE Mazishi hayo, pia yalihudhuriwa na Rais Dk. John Magufuli, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, marais wastaafu, Jakaya Kikwete, Benjamin Mkapa na Ali Hassan Mwinyi. Wengine, ni Mama Maria Nyerere, Makamu wa Rais mstaafu, Dk. Mohamed Gharib Bilal, mawaziri wakuu wa zamani, Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim, Edward Lowassa, Jaji Mkuu mstaafu, Othman Chande, Jaji mstaafu, Mark Bomani na Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma. Pia walikuwapo Balozi Paul Rupia, Balozi Job Lusinde, Spika wa Bunge mstaafu, Pius Msekwa, mwanasiasa mkongwe, Dk. Crisant Mzindakaya, Profesa Issa Shivji, Profesa Mwesiga Baregu na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku. Awali akihubiri katika ibada ya maziko, Katekista George Wilbard wa Parokia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema ili kumuenzi mwanasiasa huyo, ni vema kuishi katika yale aliyoyaamini. “Ikiwa tunaamini kwamba Yesu alikufa, vivyo hivyo wao waliolala katika Yesu Mungu atawaleta pamoja nao. Maneno haya yadhihirike kwetu leo (jana), tunapomuaga Kingunge, tuna huzuni, tumempoteza na hatutamuona tena. “Tukitaka kumuenzi ni kuishi yale aliyoyaishi na kuyafanya, kwa kufanya hivyo tutakuwa tunamwombea,” alisema Wilbard. Kwa upande wake, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Vedasto Ngombale (CUF), alisema wamepata pengo kubwa ambalo halitazibika. WASIFU WA KINGUNGE Msemaji wa familia, Balozi Ali Mchumo, alisema Kingunge alizaliwa Mei 30,1932 katika Kijiji cha Kipatimo, Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, lakini alikulia Dar es Salaam. Alipata elimu ya msingi Shule ya Msingi Mchikichini, kisha alijiunga na Shule ya Sekondari African Special na baadae Shule ya Wavulana ya Tabora. Alisema licha ya Kingunge kuwa na ufaulu ambao ungemwezesha kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, alikataa kwenda huko na kutaka kwenda kusomea sheria nchini India. “Wakati akisubiri kwenda huko, aliajiriwa na Idara ya Public Waste (kwa sasa Wizara ya Ujenzi) kama karani, mwaka 1954 Chama cha TANU kilizaliwa na wiki moja baadae alijiunga na chama hicho. “Ili aelekeze nguvu zake zote katika kupigania uhuru, aliamua kujiuzulu nafasi yake ya ukarani mwaka 1956 na kutumika kama Katibu wa TANU,” alisema Balozi Mchumo. Historia inaonyesha wakati nchi za Afrika zilipokuwa zikipigania uhuru, Kingunge alishiriki harakati hizo akiwa mmoja wa vijana wa TANU walioshinikiza kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika. Katika maisha yake, tangu ujana wake amelitumikia taifa hadi ngazi za juu kabisa. Alishika nafasi mbalimbali nchini zikiwamo mkuu wa mkoa, mbunge, waziri na mshauri wa rais katika masuala ya siasa kwa nyakati tofauti. Alijitoa CCM Oktoba, 2015 baada ya kutofurahishwa na utaratibu uliotumika kumteua mgombea urais wa CCM mjini Dodoma Julai mwaka huo. | 3 |
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM BENKI ya I&M Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, lakini inang’ara kwa kutoa bidhaa na huduma za kipekee ambazo zinakidhi mahitaji yote ya mteja katika soko. I&M Tanzania ilitambulisha akaunti mpya ya wanawake ya Tunaweza inayotoa suluhisho kwa wanawake wa ngazi zote kuanzia mmoja mmoja, wajasiriamali hadi kikundi au taasisi. Akaunti hiyo inajitofautisha kwa kutoa huduma bila malipo yoyote, haina makato ya kila mwezi na viwango vyake vya riba vinavutia kwenye akiba. Akizungumza leo jijini Dar es Salaa, katika maonyesho hayo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo, alisema kuwa bidhaa hiyo mpya imeunganishwa kwenye mtandao wa benki wa kidijitali ili kuwapa wateja huduma bora na endelevu wakati wowote wanapohitaji. Alisema I&M Tanzania ni sehemu ya I&M Holdings Kenya iliyoanzishwa mwaka 1974 kama kampuni ya huduma za kifedha kabla baadaye kubadilishwa kuwa benki ya biashara. “Mwaka huu inasherehekea miaka kumi ya huduma zetu katika soko la Tanzania. Tunafurahi kuendelea kuhudumia wateja wetu na wateja wapya, pia tunashukuru wateja wetu na washikadau wote walioshiriki katikakuiletea benki mafanikio makubwa kwa kipindi chote cha miaka kumi kwenye soko.” “Tunatoa huduma kadhaa za kifedha ikiwa ni pamoja na akaunti ya akiba, current akaunti kwa madhumuni ya biashara, mikopo ya biashara, huduma za kubadili fedha, uhamishaji fedha kitaifa na kimataifa, huduma za kidijitali ambazo hutoa fursa kwa mteja kupata huduma za benki kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *150*32# au kupitia iClick- huduma ya benki kwa njia ya mtandao inayopatikana bila kikomo kwa saa 24,” alisema Anitha Meneja Masoko na Mawasiliano huyo wa benki hiyo, alisema kuwa pia benki yao wanatoa unafuu na urahisi wa kupata mikopo na huduma nyingine kadhaa ambazo ziliwafanya watu waliotembelea banda lake kwenye maonyesho ya Sabasaba lililopo ukumbi wa Karume, upande wa kulia wa lango la kuingilia kuhamasika na kutaka kujua zaidi kuhusu benki hiyo. “I&M inafungua milango kwa Watanzania wote kwenda kujiunga na benki inayojali mahitaji yao, iliyo tayari kuwapa huduma za kipekee za kifedha kupitia wafanyakazi wake wenye uzoefu zaidi katika kutoa huduma bora kwa wateja. “Mbali na kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba, benki hiyo inatoa huduma zake bora kupitia mtandao wa matawi yake yaliyoko maeneo ya Maktaba, Indira Gandhi, Nyerere, Kariakoo, Oysterbay pamoja na mikoani ikiwa ni pamoja na Moshi, Arusha na Mwanza,” alisema Timu ya wafanyakazi wa mauzo na idara ya masoko wa benki hiyo kutoka matawi yake ya Dar es Salaam inayoongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wapo kwenye maonyesho hayo ili kuwapa wageni na wale ambao wanataka kuwekeza katika benki inayoaminika na salama ikiwa na huduma za ATM zinazopatikana kwa saa 24. | 5 |
Kinana alisema hayo kwenye mikutano tofauti ya hadhara iliyofanyika katika Makao Makuu ya Tarafa ya Nshamba na Kamachumu, katika ziara yake ya siku mbili wilayani Muleba kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM na pia kuhamasisha uhai wa chama.“Ukiona mtu anauza kahawa yake kwingine, ni kwa sababu ya bei. Kwa maoni yangu mimi, hakuna magendo hapo wanatafuta bei nzuri,” alisema Kinana kijijini Nshamba na kushangiliwa na umati uliohudhuria mkutano wake.Aliendelea kusema, “Shamba lako mwenyewe, umepanda mwenyewe, umepalilia mwenyewe, umeweka dawa mwenyewe, ukishavuna anakuja mtu wa ushirika, anakuja serikali.”Alishauri kama mamlaka zenye dhamana zinataka wananchi wasiende kuuza kahawa yao Uganda, zikaulize nchini humo wanainunua kwa bei gani.“Lakini huwezi kumwambia mtu kahawa yake Sh elfu tano kuna mahali anaweza kupata Sh 10,000 ukamwambia usipeleke, atapeleka,” alisema.Aliendelea kuhoji, “Mbona nyanya haina magendo? Ndizi ina magendo? Kahawa ina magendo kwa sababu mbili kwa sababu bei iko chini; Tafuteni namna bei iwe juu. Mtu kahawa yake akiamua kupeleka Uganda aruhusiwe,” alisema.Alishutumu kitendo cha kubughudhi wananchi kwa kuwasimamisha barabarani kudhibiti wasisafirishe bidhaa hiyo akisisitiza, “ dawa ya kahawa si polisi wala chama cha ushirika bali ni bei ya juu.”Kwa mujibu wa Kinana, juzi alikutana na maofisa wa Mamlaka ya Kahawa mjini Muleba wakamwambia sababu za bei kubwa ya kahawa ni kodi nyingi.Alisema atachukua malalamiko hayo yote na kwenda kuona wenye mamlaka kwa ajili ya kujadili suala hilo la kodi na namna ya kuziondoa.Alimwomba Mkuu wa Mkoa asaidie katika kuondoa vizuizi na bughudha wanayopata wananchi wakati wakisaka bei nzuri ya zao lao nje ya nchi hususani Uganda.Alivitaka vyama vya ushirika, Bodi ya Kahawa na Mamlaka ya Kahawa vipunguze kodi zinazosababisha bei ya zao hilo ipungue.Akiwa kwenye mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Kamachumu, Kinana aliambiwa bei ya kahawa safi isiyo na maganda, kilo wanaiuza kwa Sh 3,000 nchini wakati nchini Uganda inauzwa takribani Sh 7,000. Kahawa yenye maganda ni Sh 2,500. | 5 |
KAMPUNI ya Kuhifadhi Mafuta ya Tanzania (Tiper) imesema gawio la Sh bilioni sita iliyotoa kwa wanahisa wake, ambao ni serikali na Kampuni ya ADDAX-ORYX GROUP ya Uswisi, ni ongezeko kutoka kiwango cha Sh bilioni moja iliyotoa katika miaka ya mwisho ya 2000.Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi hisa kwa serikali ambayo ilipewa Sh bilioni tatu, Mwenyekiti wa bodi wa kampuni hiyo, Profesa Abdulkarim Mruma amesema, kiasi hicho ni ongezeko la wastani wa karibu Sh bilioni mbili katika kipindi cha kati ya mwaka 2010 hadi 2013.“Uongozi wa kampuni unaona fahari kubwa kuweza kusimamia uendeshaji na kuweza kukuza gawio kwa wanahisa wake,’’ amesema.Akizungumzia mpango wa upokeaji wa mafuta kwenye ghala moja, ambapo kampuni hiyo inatarajia kuwa kituo pekee cha upokeaji wa mafuta yote yanayoingia nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam, Prof Mruma amesema manufaa yanayotarajiwa kupatikana kutokana na mpango huo yameshajadiliwa na kupokewa vyema na wadau wote.“ Faida za mpango huu zipo wazi ambazo ni pamoja na udhibiti bora wa kiwango cha mafuta kinachoingia nchini, kupunguza upotevu na wizi wa mafuta, kuzifanya gharama za ucheleweshaji wa meli zinazolipwa sasa kwa wamiliki wa nje wa meli kuwa mapato ya serikali.’’Amesema ili kufanikisha mradi huu, Bodi ya Wakurugenzi ya TIPER imepitisha mpango mahususi wa uwekezaji wa zaidi ya dola za Marekani milioni ishirini na mbili ndani ya kipindi cha 2018 mpaka 2019.“Tumeazimia kuongeza uwezo wa kuhifadhi mafuta kwa asilimia 50 kutoka mita za ujazo 213,000 mpaka meta za ujazo 319,000 kwa kujenga matangi mawili mapya yenye mita za ujazo 80,000 kila moja na kukarabati tangi moja lililokuwa la mafuta ghafi lenye ujazo wa mita za ujazo 46,000.’’Ametaja azimio lingine kuwa ni kutandika bomba la pili la mafuta ya petroli kati ya Kurasini na Kigamboni, kuongeza uwezo wa kusukuma mafuta kwa zaidi ya asilimia 50 kwa kujenga kituo kipya cha kusukumia mafuta ambacho kitakuwa na mashine sita mpya na kukarabati mfumo wa kuzima moto ili kuweza kuongeza kiwango na kufikia viwango vinavyokubaliwa kimataifa ili kuhakikisha mafuta yako salama ndani ya ghala la TIPER.“Mpango huu wa upanuzi wa ghala unafanikishwa kwa fedha inayotokana na mapato ya ndani pamoja na mkopo wa dola milioni 15 kutoka benki,’’ ametaja.Amesema mafanikio ya mradi huo, yatakuwa ni chanzo cha kushughulikia miradi mingine kama Ghala Maalumu la Forodha, ambalo litavutia mafuta mengi kuingia nchini ili kuboresha nguvu ya ushindani na kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa bandari, mkakati itakayovutia uingizaji wa kiwango kikubwa cha mafuta kwa ajili ya biashara ya nchi jirani katika ukanda huu. | 5 |
NA AZIZA MASOUD -DAR ES SALAAM MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wamiliki wa vituo vya mafuta kutekeleza agizo la kununua na kufunga mashine za kielektroniki za risiti (EFP’s) na si kutafuta visingizio vya bei. Kauli hiyo imetolewa wakati TRA ikiwa imevifungia vituo vya mafuta ambavyo havina mashine hizo, huku baadhi ya wamiliki wakilalamikia kuuzwa kwa bei ya juu kati ya Dola za Marekani 2,500 na 3,000. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi, Richard Kayombo, alisema vituo ambavyo watavifungulia ni vile ambavyo vitafunga mashine hizo na si vinginevyo. Kayombo alisema wafanyabiashara wanapaswa kutekeleza agizo la kununua mashine hizo bila kutafuta visingizio kwa kuwa walishafanya mazungumzo na TRA na kutoa changamoto zao ambazo zimekwishafanyiwa kazi. “Wafanyabiashara waache kutafuta sababu, mwaka jana tulikutana nao na walituambia changamoto zao na tulishazitatua, walikuwa na muda mzuri wa kujiandaa kufunga mashine hizi,” alisema Kayombo. Alisema suala la bei nalo lilishazungumziwa na kufanyiwa kazi na sasa hakuna mashine ambayo inauzwa kwa bei iliyotajwa awali. Ingawa Kayombo alikataa kutaja bei ya sasa, lakini alisisitiza kuwa hiyo haiwezi kuwa sababu ya wao kushindwa kufunga mashine hizo. Alisema mbali na changamoto ya bei, TRA pia ilibadilisha mfumo wa matumizi kutoka mashine moja kutumia pampu moja ya mafuta hadi kufikia nne. Akizungumzia kuhusu changamoto ya upatikanaji wa mashine hizo, Kayombo alisema kwa sasa mamlaka hiyo imetoa zabuni kwa wasambazaji watano ambao wanapatikana nchi nzima. “Wasambazaji hawa wapo nchi nzima, lakini kwa muda tulioweka pia endapo kutakuwa na mfanyabiashara ambaye alishindwa kupata mashine, alikuwa na uwezo wa kufanya mawasiliano na ofisi za TRA, tungeweza kumsaidia,” alisema Kayombo. Mbali na hilo, Kayombo pia alitolea ufafanuzi vituo vilivyofungwa kwa kutofunga mashine hizo kulikofanywa Jumatano ya wiki hii, akisema kwa sasa vimeshaanza kufunguliwa. “Tumeshaanza kufungua vituo vya mafuta ambavyo vimeanza kutekeleza agizo la kufunga mashine na wengine wanaendelea na taratibu watafunguliwa mara tu baada ya kukamlisha,” alisema Kayombo. Alisema vituo vya mafuta 71 vilifungwa katika wilaya tatu za Mkoa wa Dar es Salaam na kati ya hivyo, 52 vimeshaanza kufunguliwa baada ya kuonyesha ushirikiano wa kuanza kufunga mashine hizo. Kwa mujibu wa Kayombo, katika Manispaa ya Ilala, kati ya vituo 31 vilivyofungwa, 20 vimefunguliwa wakati Manispaa ya Kinondoni, kati ya vituo 28 vilivyofungwa 23 vimefunguliwa na Wilaya ya Temeke vituo tisa vimefunguliwa kati ya 12. Uamuzi wa TRA kufunga vituo vya mafuta ulisababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa nishati hiyo, hasa kwa siku ya juzi na hivyo kushuhudiwa foleni kubwa katika vituo vichache vilivyokuwa wazi. Pengine kutokana na hali hiyo, siku ya jana kwa upande wa Jiji la Dar es Salaam hakukuwa na foleni tofauti na Jumamosi nyingine zote. Mapema mwaka jana TRA ilikutana na Chama cha Wauzaji Mafuta Rejareja (TAPSOA) na kukubaliana kuwa ufungaji wa mashine ufanywe kwa mchakato badala ya kuisha Machi Mosi. Kikao cha TRA na mawakala hao kilifanyika baada ya kuwapo kwa tangazo lililowataka wenye vituo vya mafuta nchini kuweka mashine hizo. Mwisho wa kufanya hivyo ilikuwa Machi Mosi, mwaka jana na ilidaiwa kitendo hicho kingesababisha mgomo kwa wenye vituo hivyo. Katika kikao hicho, Katibu wa TAPSOA Taifa, Tino Mmasi, alizitaja baadhi ya changamoto wanazozilalamikia kuwa ni EFDs kuuzwa Dola za Marekani 2,500 hadi 3,000. Pia alitaja changamoto ya kiteknolojia kuwa inaweza kuwakwamisha kwa kuwa mashine hizo zinapoharibika, huchukua muda mrefu mfanyabiashara kupata msaada kutoka kwa wataalamu. Kutokana na malalamiko hayo, TRA na TAPSOA walikubaliana kuwa wakati changamoto hizo zikiendelea kufanyiwa kazi, EFDs nazo zifungwe kwa awamu tatu na kusiwe na muda maalumu wa kukamilisha ili kuwapa nafasi wenye vituo vya mafuta kujiandaa. | 3 |
SHILINGI milioni 334 zimetumiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kununua gari la kubeba taka na makontena 20 ya kuweka taka.Kauli hiyo imetolewa jana na Fundi Mkuu wa Manispaa ya Tabora, Gaitan Mkweng’e wakati wa mkutano maalumu wa Baraza la Madiwani wa Manispaa hiyo wa bajeti.Amesema gari jimpya lililonunuliwa China litasaidia kukusanya na kuondoa taka maeneo mbalimbali.Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Tabora, Bosco Nduguru amesema uzalishaji wa tani kwa siku katika manispaa hiyo ni tani 120 lakini kabla ya ununuzi wa gari hilo walikusanya tani 70 kwa siku.Alisema gari hilo litafanya wawe na uwezo kumalizia sehemu ya taka ambayo ilikuwa inabaki kwa siku.Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira katika Manispaa hiyo, William Mpangala alisema ununuzi wa gari hilo jipya utasaidia kuongeza uwezo wao kwani kila tarafa itakuwa na gari lake la ukusanyaji wa taka.Diwani wa Kata ya Cheyo, Hamisi Kitumbo alisema ununuzi wa gari lingine utawezesha wakazi wa halmashauri hiyo kuishi katika mazingira safi na salama.Alisema hatua hiyo itapunguza uwezekano wa magonjwa ya mlipuko yanayotokana na mrundikano wa uchafu maeneo yasiyo rasmi yanayotupwa taka. | 3 |
Akizungumza katika mkutano wa wadau kuhusu utekelezaji wa mradi huo Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) mkoa Kigoma, Shaban Mtonda, sekta za kilimo na uvuvi zitanufaika katika utekelezaji wa mradi huo.Mtonda alisema wakati wa utekelezaji wa mradi huo wakulima wa zao la chikichi na sekta ya uvuvi itanufaika kutokana na kuwezeshwa kiteknolojia ili kuweza kupata mazao mengi ya uvuvi na uzalishaji hadi utayarishaji wa mafuta ya mawese huku wafanyabiashara wakiwezeshwa mitaji ya kuendeleza biashara.Kwa sasa Mtonda alisema kuwa mradi huo utatekelezwa katika wilaya za Kigoma na Kasulu ambapo pamoja na mambo mengine umelenga kubaini na kupunguza vikwazo vya kibiashara vinavyowakabili wadau katika makundi hayo kuona namna gani wanatumia fursa la soko la mpakani.Kwa upande wake mmoja wa wadai waliohudhuria mkutano huo, Ramadhani Joel alisema kuwa bado wananchi wa mkoa Kigoma hawajaweza kutumia fursa la soko la mpakani na nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu kutokana na kutokuwa na taarifa za biashara gani wanaweza kufanya na nchi hizo na nini wafanye kuweza kuingiza katika nchi kufanya biashara hizo. | 5 |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amewataka watanzania kuendelea kuishi katika umoja na mshikamano kama nguzo kuu ya maendeleo nchini.Rais ametoa wito huo leo Jijini Dar es Salaam katika hafla ya mashindano maalumu ya usomaji wa Quran barani Afrika yanayoandaliwa na taasisi ya Al-Hikma yaliyofanyika uwanja wa Taifa.Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na serikali, kitaifa na kimataifa akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Rais Mstaafu awamu ya nne Jakaya Kikwete, Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, Waziri kutoka Saudi Arabia, Sheikh Saleh Bin Abdulaziz Alsheikh, Mabalozi wa nchi mbalimbali wajumbe wa Baraza la Mawaziri, na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.Akihutubia umati uwanjani hapo Rais Magufuli amewataka watanzania kuendelea kuishi kwa amani na mshikamano kwa kuwa masuala ya dini yanamgusa kila mtu huku akiwatakia waumini wa kiislamu kuendelea na mfungo wa ramadhani kwa amani.“Kwa niaba yangu binafsi na kwa niaba ya serikali, naomba kuendelea kuwatakia kheri ya mfungo waumini wote wa dini ya kiislamu uwe wa amani” amesema RaisAkielezea changamoto ambazo zinapatikana katika kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, Rais Magufuli, ameelezea suala la upandishaji wa bei za bidhaa na kuwataka wafanyabiashara kuacha tabia hiyo kwa kuwa ni kinyume na mapenzi ya Mungu.“Ninawasihi sana watu wa aina hiyo kuacha kufanya hivyo… huwezi kutajirika kwa kutegemea kupandisha bei za bidhaa katika kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Nitoe wito kwa mamlaka husika za serikali kufuatilia jambo hili kwa ukaribu zaidi” amesema Rais Magufuli.Rais Magufuli pia ameelezea juu ya uhusiano mkubwa uliopo baina ya serikali ya Saudi Arabia na Tanzania huku akiweka wazi mipango mbalimbali iliyofikiwa baina ya nchi hizo ikiwemo ujenzi wa chuo cha kiislamu nchini.Sambamba na hilo ametoa maagizo kwa Waziri TAMISEMI, Seleman Jaffo, kutoa kibali cha utoaji wa kiwanja cha kujenga kituo cha Afya kinachotarajiwa kujengwa na taasisi hiyo.Rais ameipongeza taasisi ya Al Hekma kwa mchango wao mkubwa katika Taifa la Tanzania kwa kujenga misikiti 50, kuchimba visima 110 huku ikisomesha yatima wapatao 400.Kwa upande wake Rais Mstaafu wa Awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete amemshukuru Rais Magufuli kwa kuitikia wito huo na kuongeza kuwa ujio wake unathibitisha utanzania wa kweli ambao hautenganishwi na udini kwa kuishi katika umoja na mshikamano pasipo kufungamana na upande wowote.Naye Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi ambaye ni mlezi wa taasisi hiyo amempongeza na kumwombea Rais Magufuli aendelee na kasi yake ya maendeleo na kuwatumikia Watanzania kwa moyo. | 3 |
KIUNGO mshambuliaji wa Mbeya City Idd Selemani (pichani) amesema timu yoyote iwe Simba au Yanga ikimuhitaji ijitokeze kufanya naye mazungumzo. Mchezaji huyo mkataba wake unaelekea ukingoni mwishoni mwa msimu huu ambapo alisema hakuna timu yoyote aliyofanya nayo mazungumzo mpaka sasa.Akizungumza juzi, Selemani alisema timu yoyote itakayomuona na kuvutiwa na kipaji chake basi hawana budi kujitokeza kumalizana. “Ni kweli mkataba wangu unaelekea mwishoni na sijafanya mazungumzo yoyote, natarajia timu yoyote wakiniona na kuvutiwa na kiwango changu waje tuyamalize,”alisema.Mchezaji huyo aliifungia timu yake bao la 10 juzi katika mchezo dhidi ya Coastal Union uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya na kuwapa matumaini ya kuendelea kubaki kwenye Ligi Kuu msimu ujao.Selemani amekuwa mwiba hasa kwa timu ngumu na kuipatia timu yake matokeo. Aliwahi kuifunga Yanga mara mbili msimu uliopita walipotoka sare ya bao 1-1 na yeye ndiye aliyesawazisha. Msimu huu aliifungia timu yake bao la kufutia machozi Yanga ilipoibuka na ushindi wa 2-1.Na pia aliifungia timu yake bao moja katika mchezo dhidi ya Simba, wekundu hao walipoibuka na ushindi wa mabao 2-1. Alisema atafurahi kuona Mbeya City haishuki daraja na watapambana katika mechi za mwisho kuiwezesha timu yake kusalia kwenye ligi angalau katika sita bora. | 4 |
MABINGWA wa kihistoria Yanga wanatarajiwa kucheza mchezo wa kirafi ki na AS Vita ya DR. Congo katika kilele cha wiki ya wananchi ‘Kubwa kuliko’ Agosti 4, mwaka huu kwenye uwanja wa taifa, Dar es Salaam.Akizungumzia wiki hiyo ya wananchi Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela alisema wataanza rasmi Julai 28 kwa shughuli za kijamii kisha katika sherehe za kilele watacheza mchezo huo maalum kwa ajili ya kuwatambulisha wachezaji wapya waliosajiliwa msimu huu. “Kwa muda mrefu hatujakutana kwa pamoja hivyo tutatumia siku hiyo kukutana na wananchi kwa ajili ya kutambulisha kikosi cha msimu kuelekea kwenye maandalizi ya Ligi Kuu,”alisema.Alisema AS Vita imethibitisha kuwasili nchini Agosti 2, mwaka huu wakiwa na watu 37 na mashabiki wao na siku inayofuata watafanya mazoezi kwa maandalizi ya mchezo huo. Katika kujiandaa na mchezo huo, tayari kikosi cha Yanga kiko Morogoro kikijiandaa na msimu mpya. Katika hatua nyingine, Mwakalebela alisema Kampuni ya GSM imeshinda tenda ya kuwa msambazaji wa vifaa vyao vya michezo.“Tuliangalia tutanufaika vipi, tukaona GSM imezidi vigezo kuliko wengine, watakuwa ndio wasambazaji wakubwa wa vifaa vya Yanga, nawahimiza wanachama wasinunue jezi feki bali kununua zile zitakazosambazwa nao,”alisema.Mbali na hilo, Kaimu Katibu Mkuu Dismas Ten amewaita viongozi mbalimbali wa matawi wa klabu hiyo katika mkutano utakaofanyika Jumatano kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali. “Tunawaalika wenyeviti na makatibu wa matawi kuja katika mkutano na viongozi wa klabu Jumatano ijayo, kujadili masuala mbalimbali.Tunatarajia pia kuwaandalia vitambulisho maalum vya kuwatambua ili kuepukana na watu feki,”alisema. Wakati huohuo klabu hiyo imeachana na Kocha wake wa makipa Juma Pondamali na nafasi yake kuchukuliwa na kipa wa zamani wa timu hiyo Manyika Peter atakayeanza kazi hiyo kuanzia msimu huu. | 4 |
Erick Mugisha -Dar es salaam MKAZI wa Mwananyamala B, Mustafa Mohamed (36) amepandishwa kizimbani Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam kwa kosa la ubakaji wa mtoto wa miaka saba. Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Benson Mwaitenda, akimsomea hati ya
mashtaka mtuhumiwa mbele ya Hakimu Simon Swai, alidai kati ya Februari 2019 na Oktoba
10, 2019 eneo la Mwananyamala Kisiwani wilayani Kinondoni, Dar es Salaam
alimbaka mtoto wa miaka saba. Mshtakiwa alikana kutenda kosa na mwendesha mashtaka wa Jamhuri alidai
upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba mahakama kumsomea hoja za awali. Mwaitenda alimsomea mshtakiwa mashtaka manne ambapo alikubali hoja tatu
na kukana kosa la tatu. “Mshtakiwa nimemsomea hoja zote
nne za awali na kukubali hoja namba moja, mbili, nne na kukataa kutenda hoja
namba tatu, hata hivyo naomba mahakama tarehe nyingine kwa ajili ya kuleta
mashahidi wa kesi hiyo,” alidai Mwaitenda. Hakimu Swai alisema dhamana kwa mshtakiwa ipo wazi kwa kuwa na
wadhamini wawili waaminifu wenye barua za utambulisho, nakala ya kitambulisho
cha taifa na kusaini bondi ya Sh 2,000,000.
Mshatakiwa alitimiza masharti ya dhamana na kesi hiyo imeahirishwa hadi
Novemba 28, itakapokuja kwa ushahidi. | 3 |
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangala amewaita wawekezaji kuja nchini kwa ajili ya kuwekeza katika sekta ya utalii, wakati aliposhiriki Kongamano la 10 la Uwekezaji na Biashara katika Sekta ya Utalii Afrika.Kongamano hilo limefanyika katika Jiji la Madrid nchini Hispania, likiwa limeandaliwa na Shirika la Utalii la Umoja wa Mataifa (UNWTO) kwa kushirikiana na Taasisi za Casa Afrika na Taasisi ya Maonesho ya Biashara ya Madrid (IFEMA) na kushirikisha nchi mbalimbali duniani.Katika kongamano hilo, Waziri Kigwangala alipata fursa ya kuwa mmoja wa wazungumzaji na aliwahakikishia wawekezaji wenye nia ya kuja kuwekeza nchini kuwa ni sehemu salama ukizingatia hali ya amani na utulivu iliyopo nchini, lakini pia kuna vivutio vingi vya utalii na fursa za kuwekeza.“Nawakaribisheni nyote, njooni Tanzania muwekeze kutokana na uwepo wa mazingira na miundombinu bora kwa ajili uwekezaji katika sekta ya utalii pamoja na viwanda,”amesema.Waziri Kigwangala pia alitumia nafasi hiyo kutangaza ukanda mpya wa Kusini mwa Tanzania ambao umejaliwa kuwa na vivutio vya utalii vya kipekee vinavyopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Mikumi na Pori la Akiba Selous.Katika hatua nyingine, Waziri Kigwangala aliwaeleza washiriki hao kuhusu juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali ya inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa kutaja mifano michache kama vile kufufua Kampuni ya Ndege (ATCL) kwa kununua ndege mpya saba, pamoja kujenga chanzo kikubwa cha kuzalisha umeme katika mto Rufiji cha Stigler’s Gorge. | 5 |
Wakati Simba wakipania kushinda kwenye uwanja huo wa ugenini, watu wanajiuliza maisha ya Mbeya City yatakuwaje bila ya kocha wao Juma Mwambusi aliyeipatia timu hiyo mafanikio makubwa. Mwambusi kwa sasa ni kocha msaidizi wa Yanga aliyechukua mikoba ya Charles Mkwasa aliyepewa mkataba wa mwaka mmoja na nusu wa kuifundisha timu ya taifa,Taifa Stars.Ni mchezo ambao sio tu unapima uwezo wa aliyekuwa msaidizi wa Mwambusi, Abdul Mingange bali pia watu wanataka kuona ujio wa mchezaji wa zamani wa Simba Haruna Moshi ‘Boban’ aliyejiunga na timu hiyo hivi karibuni kama utasaidia kikosi hicho cha Mbeya kupata pointi.Tayari Simba walifanikiwa kuvunja mwiko katika uwanja wa Mkwakwani Tanga na kusema kuwa hata Mbeya itakuwa hivyo hivyo kwani walitambia kikosi chao kuwa kimefanya maandalizi ya kutosha kushinda.Simba imejitahidi kuanza msimu vizuri, ambapo katika michezo mitano waliyocheza, wamepoteza mmoja na kushinda iliyobaki hivyo wana pointi 12 nyuma ya Azam FC na Yanga zenye pointi 15 kila moja. Mbeya City ilianza vibaya msimu huu, ambapo katika michezo sita waliyocheza wameshinda mmoja, sare moja na kufungwa mara nne.Utakuwa ni mchezo mgumu kwa kuwa kila mmoja anahitaji matokeo mazuri huku Kocha Abdul Mingange akisema kuwa kikosi chake kiko vizuri na kimejipanga kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani kubakiza pointi tatu.Kocha wa Simba, Dylan Kerry alitamba kuwa kama waliweza kushinda michezo migumu ya Tanga, ni lazima wapate pointi tatu dhidi ya Mbeya City.Simba huenda ikamkosa nyota wake Hamis Kiiza na Emery Nimuboma wanaosumbuliwa na majeraha na Mbeya City itamkosa Juma Nyosso aliyefungiwa kucheza soka kwa miaka miwili kutokana na kosa la kinidhamu, lakini ikijivunia kuwa na wachezaji wazoefu kama Haruna Shamte, Juma Kaseja na Boban.Mbeya City inatambia wachezaji wake wawili waliowahi kutamba na Simba, Boban na kipa Juma Kasema, ambao wamepania kuhakikisha timu yao hiyo ya zamani leo haitoki kwenye uwanja huo wa Kumbukumbu ya Sokoine.Michezo mingine ya Ligi Kuu leo Jumamosi ni Majimaji FC dhidi ya African Sports ya Tanga katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea, Ndanda FC wakiwakaribisha Toto African katika dimba la Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.Stand United watawakaribisha Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyaga, huku Coastal Union ya Tanga watakua wenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Mkwakwani.Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumapili wakati maafande wa Mgambo Shooting watakua wenyeji wa Kagera Sugar uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, huku wachimba almasi Mwadui FC wakiwakaribisha JKT Ruvu inayoshika mkia katika msimamo wa ligi hiyo. | 4 |
Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA
HATIMAYE Baraza la Madiwani la Manispaa ya Dodoma limemng’oa Meya wa Manispaa hiyo, Japhari Mwanyemba (CCM), kwa tuhuma za kutafuna Sh milioni 30 za mradi wa maji katika eneo la Zuzu katika manispaa hiyo.
Fedha hizo zilizotolewa na Ubalozi wa Japani kwa aliyekuwa Mke wa Waziri Mkuu, Tunu Pinda kwa ajili ya mradi huo.
Madiwani hao ambao kwa pamoja walipiga kura za kutokuwa na imani na Mwanyemba katika kikoa maalumu cha baraza hilo kilichofanyika jana mjini hapa.
Zoezi hilo ambalo liliongozwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma, Godwin Kunambi, akishirikiana na Naibu Meya wa Manispaa hiyo, Jumanne Ngede.
Pia zoezi hilo lilishuhudiwa na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, Mbunge wa Viti Maalumu Felister Bura na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Christina Mndeme.
Sekeseke hilo lilianza baada ya mkurugenzi kumaliza kusoma ripoti ya tume iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana kuchunguza fedha za mradi huo wa maji kutowaridhisha baadhi ya madiwani.
Mkurugenzi huyo alitumia zaidi ya saa nane kuisoma ripoti hiyo huku wajumbe wakiwa wapole na wengine wakionekana kuguswa kwa hisia kali.
Naibu Meya Ngede aliagiza kupigwa kwa kura za siri ambapo kati ya madiwani 56 waliohudhuria baraza hilo 43 walipiga kura ya kutokuwa na imani na mwenyekiti huyo.
Akitangaza matokeo Mkurugenzi wa manispaa hiyo Kunambi alisema madiwani 8 waligomea zoezi hilo na kutoka nje huku wane wakipiga kura ya kuwa na imani na meya huyo na 43 wakiunga mkono kumng’oa.
“Natangaza kwa mujibu wa kanuni za Halmashauri kifungu namba 4 kanuni ndogo ya nane kuanzia mida hii majira ya saa 8.30 mchana waheshimiwa madiwani natangaza rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Dodoma sio Mstahiki tena,’’alisema Kunambi huku akishangiliwa. | 3 |
Na TUNU NASSOR, DAR ES SALAAM HOFU ya kuenea magonjwa ya mlipuko ikiwemo Dengue na Kipindupindu imetanda kwa wakazi wa mtaa wa Mtambani A Kata ya Jangwani Manispaa ya Ilala kutokana na kukithiri kwa uchafu katika mazingira ya eneo lao. MTANZANIA JUMAPILI lilifika katika mtaa huo na kubaini kuwapo kwa uchafu uliokithiri ikiwamo maji yaliyotuama ndani na nje ya baadhi ya nyumba zao kwa muda mrefu. Maji hayo ambayo wakazi hao wanasema yametuama kwa takribani miaka minne tangu kilipojengwa kituo cha mwendokasi yalionekana kubadilika rangi kutokana na kuchanganyika na yale yaliyotoka katika vyoo. Gazeti hili lilishuhudia baadhi ya nyumba zikiwa zimezingirwa na tope hali iliyofanya watu wapite kwa tabu katika maeneo hayo. Pamoja na nyumba nyingi za mtaa huo kuzungukwa na maji ambayo yanatoa harufu mbaya, pia maeneo yote ya mtaa huo yamezungukwa na uchafu ikiwamo mifuko chakavu ya plastiki maarufu. Mwandishi wa gazeti hili alizungumza na mkazi wa eneo hilo liyejitambulisha kwa jina la Halima Said ambaye alionekana akitoka katika tope hilo na kuingia katika nyumba ambayo imejaa maji. Mama huyo ambaye mtoto wake alilazwa katika Hospitali ya Amana kutokana na ugonjwa wa kuhara alisema nyumba iliyojaa maji ndio anayoishi kwa sasa. “Humu ndani ndimo ninaishi na hali hii kwa sasa tumeizoea kwa kuwa imekuwa ya muda mrefu,” alisema Halima. Alisema maji hayo yamekuwapo kwa muda mrefu ambapo awali walilazimika kukimbia makazi hayo kuepuka mafuriko lakini mvua zilipopungua waliamua kurejea. “Tumerejea hapa ndio tumekutana na maradhi ya Dengue na Kipindupindu, tuliondoka kwa mafuriko tumerudi tumekuta maradhi,” alisema Halima. Naye Mwenyekiti wa mtaa huo, Ally Mohamed alisema hata ofisi ya serikali ya mtaa huo imejaa maji kwa takribani miaka minne jambo lililosababisha viongozi hao kufanya shughuli zao nje. “Kama mlivyoona hapa tangu miundombinu ya maji ya eneo hili kuzibwa na maji kushindwa kuelekea baharini imekuwa mateso kwa wakazi wetu,” alisema Mohamed. Wakati hali ikiwa hivyo katika eneo hilo Manispaa ya Ilala imeanza kupulizia dawa ya kuua viruirui na mbu wa Dengue na wadudu wanaosababisha Kipindupindu. Wagonjwa wanane wa kipindupindu wameripotiwa katika eneo hilo. | 0 |
RAIS John Magufuli ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, kuwasaidia wawekezaji wazawa ili waweze kujenga viwanda. Pia amewataka wakazi wa Ukerewe mkoani Mwanza, kushirikiana na serikali ili kuijenga Tanzania mpya yenye uchumi imara. Aliyasema hayo katika mikutano aliyoifanya katika maeneo ya Magu na Ukerewe mkoani Mwanza akiwa katika ziara ya kutembelea mikoa ya Kanda ya Ziwa.Akizindua kiwanda cha Lakairo Industries Group Limited kilichopo wilayani Magu mkoani Mwanza, Rais Magufuli aliziagiza wizara hizo mbili kuwasaidia wawekezaji wazawa ili waweze kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa viwanda. Alitoa mfano kuwa Mbunge wa Rorya mkoani Mara, Lameck Airo ni mfano wa kuigwa kwa wawekezaji wazalendo katika kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda na aliwataka wabunge wengine kuiga mfano wake.Akiwa Ukerewe, Rais Magufuli aliwataka wakazi wa kisiwa hicho, kushirikiana na serikali ili kuijenga Tanzania mpya yenye uchumi imara. Alisema katika kutekeleza sera ya maendeleo serikali yake imeanza kuiandaa Tanzania ya neema kwa kuwabana wezi, mafisadi na wala rushwa, ambao wamekuwa kikwazo kwa maendeleo ya nchi kwa muda mrefu. Alitolea mfano wa fedha zilizokuwa zikipotea kuwalipa wafanyakazi hewa, lakini kwa sasa zimeokolewa na zinatumika kwenye ununuzi wa ndege, kujenga miundombinu za usafiri wa gari, treni na shughuli nyingine za maendeleo.Alisema: ”Miradi mikubwa ya umeme kama vile Stiegler’s Gorge, mradi wa usafiri wa kisasa wa treni ya Standard Gauge itakayoanzia Dar es Salaam kuja Mwanza kupitia Dodoma itatekelezwa tena kwa fedha za kodi zenu. Kwa sasa tumejipanga kuifanya Tanzania kuwa mpya na yenye neema, ni jukumu lenu na nyie kufanya yale yaliyo ndani ya uwezo wenu kuendeleza Ukerewe na serikali itawasaidia. Hivi iweje viwanda vya nguo na uwekezaji mwingine unapotea tu, sasa basi ni lazima tujipange kurekebisha hali hii,” alisema.Alisema, katika kuwafikishia neema mkoani humo, serikali imenunua meli ya kisasa itakayobeba abiria na mizigo kwa bei ya kawaida ili kuwapatia fursa wakazi wa Mkoa huo wakiwamo hao wa Ukerewe kufanya biashara. Aliongeza, miradi ya umeme ya Kinyerezi 1,2,3 na 4 inazalisha megawati za umeme 2,263 zitakazokuja kuongezewa nguvu na Stiegler’s Gorge ambao ukikamilika utazalisha megawati 2, 265 na hivyo nchi kuwa na umeme wa megawati 4,263, ambazo zinatosha kuendesha viwanda. Pia aliwataka viongozi wa serikali, kuacha kufanya kazi kwa kutaka sifa, badala yake wawe na mikakati endelevu itakayowawezesha viongozi hao kuwahudumia wananchi. Leo Rais Magufuli anaendelea na ziara yake mkoa wa Mara, ambapo atakagua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi. | 3 |
Juzi Tiboroha alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo hali ambayo imezua mtafaruku mkubwa kwa wanachama wa klabu hiyo, ambao baadhi yao hawataki ajiuzulu. Manji jana alizungumza na waandishi wa habari na kuweka wazi suala hilo la kuondoka kwa Tiboroha.Alisema kuwa hali ya kutokuelewana na katibu huyo ilitokana na sakata la mchezaji Niyonzima, ambapo alisema kuwa katibu huyo alikuwa na chuki binafsi na mchezaji huyo akitaka afukuzwe kuichezea Yanga.Alisema kuwa Tiboroha alificha taarifa muhimu za mchezaji huyo kutoka Shirikisho la Soka la Rwanda (Ferwafa) zilizotumwa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) kuhusiana na kuchelewa kwa mchezaji huyo kuichezea.Alisema kuwa badala yake aliendesha kampeni kuwa mchezaji huyo amechelewa bila ya taarifa hali iliyosababisha kuonekana kuwa hana nidhamu.Alisema kuwa sio kawaida kwa mchezaji mwenzake Niyonzima anayechezea Azam FC ambaye barua yake ilipokelewa na klabu ya Azam, lakini ile ya Niyonzima kuja Yanga ilipokelewa na Tiboroha na hakuiwasilisha kunakohusika ili kumharibia mchezaji huyo.Alisema kuwa hali hiyo ilikuwa ni kutokana na chuki binafsi kutoka kwa katibu huyo hali ambayo ilizua hali ya chuki kwa mchezaji huyo dhidi ya mashabiki na wachezaji wenzake kwa ujumla.Manji alisema kuwa, hiyo ni moja kati ya mambo mengi ambayo katibu huyo amekuwa akiyafanya, ambapo amekuwa akificha uozo wake huo kwa kujidai kuwa yeye ni mtendaji mwema huku akitumia baadhi ya vyombo vya habari kumtetea na kumsafisha.Alisema kuwa ndani ya miezi 12 ya uongozi wake amechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa kasi mapato ya klabu hiyo huku matumizi ya klabu yakizidi kupanda mara nne kutoka milioni 500 kwa mwaka hadi kufikia bilioni 2.“Kabla yake klabu ilikuwa imekaribia kujikomboa na kuanza kujitegemea, lakini alipofika aliamua kujishirikisha kwa ukaribu zaidi na TFF na kukubaliana nao karibia kwa kila kitu na kujikuta akishusha mapato ya klabu,” alisema Manji.Alisema kuwa katibu huyo alikuwa kwa maslahi yake binafsi huku akichukua kila fursa ambayo ilikuwa inaenda klabuni hapo kwa maslahi yake binafsi.Alisema kuwa Yanga ilialikwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa, FIFA, kwenye semina ya mafunzo iliyofanyika nchini Ghana, lakini katibu huyo alijichagua mwenyewe bila ya kushirikisha Kamati ya Utendaji, alichukua cheti cha ugonjwa na kisha akajidai anaumwa, lakini akasafiri kwenda kwenye mafunzo hayo.Alisema kuwa katibu huyo alimwathiri mchezaji Ngoma wa klabu hiyo kwa kumwambia kuwa anatakiwa kwenda Uturuki kwa majaribio huku mchezaji huyo akitakiwa kuwa katika michuano ya Mapinduzi hali ambayo iliathiri uchezaji wa Ngoma kwenye michuano hiyo.Alisema kuwa amesababisha kupotea kwa kitita cha dola za Marekani 5,000 baada ya kuikopesha timu ya Botswana ya BDF, lakini fedha hizo hazijarejeshwa hadi leo. Alisema kuwa alimtaka katibu huyo aandike barua ya kijiuzulu ili kulinda heshima yake baada ya kurejesha fedha hizo na katibu huyo alifanya hivyo Ijumaa iliyopita.Alisema kuwa kwa sasa nafasi yake inashikiliwa kwa muda na Mhazini wa Yanga, Baraka Deudeit huku Omar Kaya akisimamia wanachama wa klabu pamoja na kusaidia maandalizi ya uchaguzi.Alisema kuwa Jerry Muro anaendelea kuwa ni msemaji wa klabu huku Mkuu wa Kitengo cha Fedha Faidhal Mike atashirikiana na Justina atakayekuwa Mhazini msaidizi wa klabu hiyo.Alisema kuwa klabu ya Yanga itatumia kampuni binafsi kushugulikia masuala ya masoko pamoja na sheria. Alisema kuwa amemwagiza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi kuhakikisha kuwa anaandaa tarehe ya uchaguzi ikiwa pamoja na kupewa majina mapya ya kamati hiyo.Aliongeza kuwa hata kwa upande wake yeye kama Mwenyekiti wa sasa wa klabu hiyo pia atagombea nafasi hiyo. Pia Manji aligusia suala zima la kuuzwa kwa mchezaji wa klabu hiyo Kpah Sherman, kuwa ameuzwa kwa kitita cha Sh milioni 33 katika timu ya Black Aces ya Afrika Kusini. | 4 |
KUALA LUMPUR,
Malaysia MFALME wa hapa,
Muhammad V ametangaza kujiuzulu
wadhifa wake ikiwa ni mara ya kwanza tukio hilo kutokea kwa kiongozi kama huyo
kuachia madaraka kabla hajamaliza kipindi cha miaka mitano ya utawala wake. Taarifa ya mfalme huyo kujiuzulu ilitolewa
jana na kasri ya kiongozi huyo, lakini haikutaja sababu za kujiuzulu na huku
maofisa wa ofisi wakishindwa kutoa majibu. Baraza la kifalme la
hapa lina wafalme tisa na mrithi wa kio ngozi huyo anaweza kuchaguliwa na
viongozi hao. Katika taarifa hiyo
ya Kasri ilieleza kuwa mflame huyo anasema kwamba anapongeza kwa nafasi hiyo
aliyokuwa amerpewa na akawashukuru Waziri Mkuu na Serikali yake. “Kwa upeo wake
umefanya kazi ili kutekeleza majukumu yake aliyopewa na mkuu wa serikali, akiwa kama nguzo ya
utulivu, chanzo cha haki, msingi wa umoja kwa ajili ya watu wote wa taifa
hili,” taarifa hiyo ya kifalme ilieleza bila kutaja sababu za kuachia
kwake madaraka.. Hata hivyo kujiuzu kwa mfalme huyo kumekuja
ikiwa ni takribani wiki moja tangu aanze kazi, baada ya kutumia muda wa miezi
miwili akiwa nje ya nchi kwa ajili ya likizo ya matibabu. | 2 |
MONROVIA: Liberia WANANCHI wa Liberia walipiga kura jana kuchagua rais ambaye atakuwa badala ya rais wa sasa mwanamke na mshindi wa Nishani ya Amani ya Nobel, Ellen Johnson Sirleaf. Mwanasoka wa zamani, George Weah (51) na Makamu wa Rais, Joseph Boakai ndiyo washindani wakubwa wa urais katika uchaguzi huo. Liberia, ambayo ilianzishwa katika Karne ya 19 na waafrika waliokuwa watumwa Marekani haijawa na mabadiliko ya amani ya madaraka ya urais kwa miaka 73. Sirleaf aliwataka wananchi kushiriki katika uchaguzi huo kwa amani katika nchi hiyo ambayo iliwahi kukabiliwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa miaka 14. “Kura yako ni kuhusu wewe na familia yako – siyo chama, ukabila,” alisema katika hotuba yake kwa taifa. Watu wapatao 20 wanagombea urais katika uchaguzi huo. Hao ni pamoja na Alex Cummings, ofisa mkuu wa zamani wa Kampuni ya Coca-Cola, na MacDella Cooper, mwanamitindo wa zamani na rafiki wa zamani wa kike wa Weah. Sirleaf (78), hagombei tena baada ya kumaliza uongozi wake wa mihula miwili. Alishika madaraka mwaka 2006 baada ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Charles Taylor, kulazimishwa kuachia madaraka mwaka 2003 na waasi waliokuwa wanaipinga serikali yake. Hivi sasa Taylor anatumikia kifungo cha miaka 50 Uingereza kwa makosa ya vita yanayohusiana na vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Sierra Leone. | 2 |
NA LAMECK KUMBUKA, Geneva, Uswisi KITENDO cha wananchi wa Taifa la Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya kimeleta madhara makubwa. Kama wasemavyo vijana wa siku hizi muziki wa ‘Brexit’ sasa si wa kitoto na hakika umeleta dhahama huko Uingereza. Tunaweza kuazima msemo uliopo kwenye wimbo wa CCM ‘wataisoma namba’ ndicho ambacho kinawakuta wananchi wa Uingereza. Waingereza walipopiga kura ya kujiondoa katika Jumuiya ya Ulaya (European Union), waliangalia kwa jicho chongo, hawakufikiria kwa kina athari zake. Januari 4, mwaka huu, Sir Ivan Rogers, Mwanadiplomasia nguli wa Uingereza amejiuzulu cheo chake kama balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Uingereza katika Umoja wa Ulaya (EU). Kwa maana nyingine kitendo hicho ni kama ameshtukia dili. Mjadala juu ya biashara kati ya Uingereza na Umoja wa Ulaya umegubikwa na sintofahamu. Wachambuzi wa mambo wanasema inaweza kuchukua zaidi ya miaka 10 kufikia mwafaka. Wahenga walisema ukibana vyako usitegemee utakula vya wengine kirahisi. Sir Ivan Rogers kwa lugha nyingine amesema, hawezi kukabiliana na mzigo mzito wa kujitoa EU kwa kuwa alishawatahadharisha mapema. Mwanadiplomasia huyo ametangaza kujiuzulu na kuitaka Uingereza itafute mtu mwingine aiwakilishe. Nafahamu wengi watasema suala hilo lilikuwa la kidemokrasia na wengi ndio walioshinda. Kimsingi dhana ya wengi wape imekuwa na maswali mengi kuhusu kuhalalisha demokrasia. Je, kiongozi bora au maamuzi bora ni yale ya wengi au ni yale yanayowakilisha makundi yote yatakayoguswa na hayo maamuzi? Je, kama wengi hao uwezo wao wa kufikiria ni mdogo bado watatoa maamuzi sahihi kisa ni wengi? Masuala haya yalisababisha Marekani kuja na mfumo ule wa upigaji kura wa wawakilishi wa majimbo (Electoral Vote). Hii inamaanisha kuwa kura za wananchi (Popular/Majority Vote) yaani kura za wengi haziakisi maamuzi au kiongozi bora. Mfumo wa Electoral Vote hupewa kipaumbele kwani ni kura zinazoakisi wawakilishi sehemu tofauti majimbo tofauti yanayoguswa na maamuzi haya. Ndiyo maana mgombea wa Chama cha Democrat, Hilary Clinton, akapata kura nyingi lakini hakuwa rais. Simaanishi kuwa mfumo wa Marekani ni bora au hutoa viongozi bora ila najaribu kuelezea sintofahamu na mkanganyiko juu ya dhana ya wengi wape na dhana ya demokrasia. Mantiki ya Electoral Vote kwa Wamarekani ni kuwa kama wingi wa kura utaakisi maamuzi bora au kiongozi ni kwamba tutajikuta katika siasa za ukabila na rushwa. Mfano, kabila lenye watu wengi huweza kujikuta linatoa kiongozi au wanasiasa wanaligombania kuhonga na kuligombania wakati wa kampeni. Tushukuru Mungu Tanzania tuna neema, la sivyo dhana hiyo ya wengi wape ingesababisha kila kiongozi kutoka Kanda ya Ziwa kwani kwa kuwa Wasukuma ni wengi basi anayekubalika na Wasukuma angekuwa moja kwa moja kiongozi au maamuzi yanayoungwa na watu wa Kanda ya Ziwa yangepita. Je, watu wa Kanda ya Ziwa au Wasukuma wakitaka kitu au wakimtaka fulani basi ndio sahihi? Haya ni maswali. Unaona Mungu alivyotujalia tumekuwa na marais kutoka makabila madogo sana ambao hata si maarufu maadamu wanakubalika na wote. Ona dhana ya wingi inavyoitafuna jirani Kenya. Waluo na Wakikuyu wamekuwa na msuguano miaka nenda miaka rudi hadi kukitishana huo msuguano baba yake Raila Odinga, Oginga Odinga, alipambana kamwachia kijana bado anaendelea. Pia, dhana ya wengi wape ni hatari kwa nchi ambazo hazijaendelea kama wale wengi ni mbumbumbu. Kwa lugha nyingine maamuzi ya wajinga yanakuwa maamuzi ya taifa zima. Sina nia ya kubeza dhana ya wengi wape ila najaribu kukueleza athari ya dhana ya wengi na mantiki ya demokrasia. Hii ndiyo inaitafuna Uingereza kwenye sakata la kujitoa EU yaani Brexit. Mojawapo ya masuala yaliyopeleka Brexit ni uhamiaji. Waliamini kuwa wahamiaji wanachukua kazi na fursa za wazawa Waingereza. Pia wahamiaji wengi hupitia huko Italia na suala la kubeba msalaba (Burden sharing) ndani ya Jumuiya ya Ulaya hujikuta wanabeba mzigo usio wao. Kuna suala huwa linashangaza Ulaya na nchi za Magharibi, wazee na watu wa vijijini ambako hata hakuna mhamiaji au mgeni anayeishi huko ndio wanaochukia wahamiaji. Kwa lugha nyingine chuki yao ni ya kinadharia na kibaguzi. Ni sawa na mtu anamchukia mtu ambaye hata hamjui. Nimekuwa nikiishi hapa Geneva, ni jiji kubwa ambalo limejaa wageni kutoka nchi mbalimbali ila wazawa wa jiji hilo huwa hawapigi kura kufukuza wageni. Hapo ndipo kuna wageni wengi kuliko sehemu nyingine nchini Uswisi. Vijijini ambako wageni hawapo huwa wanaandamana kupinga wahamiaji hayo ndiyo maajabu. Kwa Marekani, Mmarekani mweusi ambaye hakusoma atamchukia sana Mnigeria au Mghana mhamiaji daktari au mwanasheria aliyebobea eti kamchukulia kazi kana kwamba huyo daktari asingefanya hiyo kazi huyo Mmarekani mweusi anayeshinda anavuta bangi magetoni angefanya hiyo kazi. Vijana wengi watu wa mjini na wasomi huwa wana uwezo wa kupambanua na wako wazi kimawazo. Kwa bahati mbaya watu hao hao huwa hawako tayari kupanga mstari kwa saa mbili au tatu kupiga kura kutetea yale maamuzi yao. Watu wa vijijini wazee na wale wasio na elimu maamuzi yao mara nyingi ni ya uzoefu na ya kale ambayo wakati mwingine hayaakisi hali halisi ya maisha tuliyonayo wengi. Lakini kundi hilo ndilo watu ambao wako tayari kupanga mstari saa tatu huku mvua ikinyesha kupiga kura kwani huwa ni wanazi wa kile wanachokiamini, si wapembuzi. Yaani kama ni kwa soka ndio wale wabongo wanapigana kisa ubishi wa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo. Ndiyo maana siku ya kura ya Brexit mvua ilinyesha na watu wa jiji la London waliotegemewa kura yao iongee hawakupiga kura kwa wingi kisa mvua. Hayo ndiyo maajabu ya siasa, aliye makini ni mvivu wa kupiga kura na humwachia asiye makini aamue hatima ya maisha yake. | 2 |
NA HASTIN LIUMBA
-NZEGA
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja amemuomba Mke wa Rais Mstaafu, Mama Salma Kikwete kuutafakari kwa makini uteuzi wa ubunge alioteuliwa jana na Rais John Magufuli.
Mgeja ambaye pia ni Mwenyekiti wa taasisi inayoshughulika na utawala bora ya Tanzania Mzalendo Foundation, amesema nafasi aliyofikia mama Salma akiwa mke wa rais mstaafu na ‘First Lady’ wa nchi ni nafasi kubwa kiitifaki hivyo anapaswa kuwa na heshima na abakie kuwa mama mshauri na mlezi wa taifa.
“Namuomba Mama Kikwete aige mfano wa mama Regina Lowassa (mke wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa) ambaye wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015 na baada ya uchaguzi Chadema ilimpa heshima kwa kumteua kuwa Mbunge wa Viti Maalumu lakini kwa heshima aliikataa nafasi hiyo.
“Mke wa rais mstaafu siyo mtu au kiongozi mdogo lazima tujiulize inapotokea akachangia hoja ndani ya bunge ikapingwa au aambiwe kaa chini au toka nje au atolewe nje na askari wa bunge je, hiyo heshima au aibu na fedheha inaenda kwa nani?” amehoji Mgeja.
Pamoja na mambo mengine, Mgeja amesema wake wa viongozi ni sehemu ya viongozi ambapo ana mashaka itifaki ndani bungeni inaweza kugongana hivyo amemtaka Mama Salma Kikwete akapokea ushauri na mitazamo ya watu mbalimbali na isimaanishe kwamba anamuonea wivu kwani maamuzi yanabaki kwake kukataa ama kukubali ushauri huo kama changamoto katika kupanga na kuchagua. | 3 |
Na Walter Mguluchuma-Katavi WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inatarajia kutoa ajira kwa watumishi wa kada mbalimbali za afya. Imesema watakaopewa kipaumbele ni wale wakataoomba kufanya kazi mikoa ya pembezoni ambayo ina upungufu mkubwa wa watumishi wa sekta hiyo. Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, wakati alipokuwa akihutubia wakazi wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi na kufungua upimaji na utoaji tiba wa magonjwa yasiyoambukiza. Alisema Serikali inatarajia kutangaza ajira za watumishi 52,000 wa kada mbalimbali hivi karibuni, hivyo kwa nafasi za ajira zitakazotolewa zitagusa mikoa tisa. Alisema watakaoomba kupangiwa kufanya kazi Mkoa wa Dares Salaam hawatakuwa na nafasi ya kuchaguliwa kwanza, kwani mkoa huo hauna tatizo kubwa. Aliitaja mikoa yenye uhaba wa wataalamu kuwa ni Katavi, Rukwa, Kigoma, Simiyu, Shinyanga, Tabora, Geita na Kagera. Alisema tayari wizara yake imeandaa muswada kwa ajili ya kuupeleka bungeni ili ujadiliwe na hatimaye uwe sheria itakayowezesha kila mtu ajiunge na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Naye Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali mstaafu Raphael Muhuga, alisema Katavi ina watumishi 692 kati ya 2,174 wanaohitajika. Alisema kuna upungufu wa watumishi 1,186 sawa na asilimia 69 ya mahitaji. Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Katavi, Anna Shumbi, alisema mkoa huo unaongoza kwa mimba za utotoni. | 0 |
NAZI zinauzwa hadi Sh 100! Inashangaza lakini hii ndiyo hali halisi katika wilaya ya Mafia ambacho ni kisiwa kilichopo karibu na mlango wa Mto Rufiji. Kulingana na sensa ya mwaka 2012, wilaya hii ilikuwa na wakazi 46,438. Wakazi wa kisiwa hiki ambao wengi wanajishughulisha na uvuvi pamoja na kilimo hususani cha nazi, wamekuwa ‘wakilia’ na masoko ya zao hilo; changamoto ambayo serikali inaikabili kwa kuwekeza kwenye viwanda na usafiri. Mmoja wa watu wanaojihusisha na kilimo pamoja na biashara ya nazi, Shenaz Issa, anasema ukosefu wa soko la uhakika la zao hilo unawapa wakati mgumu kiuchumi na kijamii. Anasema kinachowaumiza ni kukosa usafiri wa uhakika na viwanda vya kusindika nazi, halia ambayo huwalazimu wakulima kuuza nazi zao kwa bei ya kutupa. Julai mwaka huu, Mkuu wa wilaya ya Mafia, Shaibu Nnunduma alipozungumza na madiwani, alithibitisha kwamba nazi zinauzwa kati ya Sh 100 na 150; kiasi ambacho hakimnufaishi mkulima. Alisema uanzishaji wa kiwanda cha nazi ndiyo utainua soko la zao hilo katika kisiwa hicho. Ofisa Mtenda wa Chama cha Wafanyabiashara, wenye Viwanda na Wakulima (TCCIA) mkoa wa Pwani, Anne Maridadi, anaunga mkono akisema kumekuwapo na kilio juu ya ukosefu wa uhakika wa soko la nazi. Maridadi anasema wakati kilimo kikihitaji uwekezaji wa kutosha, upatikanaji masoko hauna budi kutiliwa mkazo. Anasisitiza uzalishaji kwa wingi kwenye kilimo ndiyo chachu ya uwekezaji kwenye viwanda. Taarifa ya mkoa huo inaonesha kwamba Mafia ambayo ni moja ya wilaya saba za mkoa wa Pwani, inazalisha tani 35,000 za nazi kwa mwaka; kiasi ambacho ni kikubwa. Wilaya nyingine zinazounda mkoa wa Pwani ni Kibaha, Bagamoyo, Kibiti, Rufiji, Mkuranga na Kisarawe. Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo anasema baada ya kubaini kuwapo uzalishaji mkubwa wa nazi usio na soko, juhudi zinafanyika kuhakikisha changamoto hiyo inakwisha. Ndikilo ambaye alikuwa akizungumzia maonesho ya biashara na kongamano la uwekezaji la mkoa wa Pwani litakalofanyika mwezi ujao, anaeleza mikakati ya kufungua kisiwa cha Mafia kiuchumi. Mikakati hiyo anasema inahusisha uboreshaji wa usafiri wa majini na anga kuhakikisha wilaya hiyo inafikika kirahisi. Mkakati mwingine ni kukaribisha wawekezaji wa viwanda vikiwamo vyenye uhusiano na kilimo, mathalani cha kusindika nazi.“Ndiyo maana Juni mwaka huu balozi wa Tanzania nchini Malaysia alikuja na wawekezaji na kuchukua mwongozo wa mkoa wa uwekezaji. Wanajipanga kuanzisha kiwanda kikubwa cha kuchakata nazi,” anasema. Mwongozo huo wa uwekezaji umetayarishwa na Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) ofisi ya Tanzania. Mwongozo huo utakaozinduliwa rasmi kwenye Kongamano la Fursa za uwekezaji na Biashara litakalofanyika Oktoba 3, 2019, umeainisha fursa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa huo. Ndikilo ametaja baadhi ya fursa hizo kuwa ni sekta ya kilimo, uvuvi, utalii, ujenzi wa viwanda na huduma za jamii. Ndikilo anasema mkoa umejiridhisha yaliyomo katika mwongozo ndiyo Mafia picha halisi ya Pwani. Ndikilo anasema serikali kupitia mwongozo huo inaainisha fursa kwa ajili ya wawekezaji wa viwanda vikiwapo vya kuchakata samaki ikizingatiwa kwamba asilimia 90 ya mapato ya Mafia yanatokana na uvuvi. Anasema nazi ambalo ni zao lenye matumizi yapatayo 70, likitumika vizuri lina uwezo wa kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla. Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo (TARI) cha Mikocheni, Dar es Salaam, Dk Zuberi Bira anathibitisha zao hilo lilivyo na faida nyingi. Wakati wa maonesho ya Nanenane yaliyofanyika mkoani Simiyu mwaka huu, Dk Bira alitaja faida mbalimbali za nazi ikiwamo kutoa mafuta yenye matumizi mbalimbali. Faida nyingine alisema ni mnazi kutumika kama mbao, makuti kujengea nyumba na vifuu vya nazi kutengeneza vitu mbalim bali yakiwamo mapambo. Baada ya kufua nazi, mabaki pamoja na majani ya minazi yanaweza kutengeneza mbolea. Maji ya nazi changa ‘madafu’ hutumika kama kinywaji. Usafiri wa uhakika unatajwa kuwa kivutio kikubwa cha uwekezaji katika zao hilo la chakula na biashara na ndiyo maana mkuu wa mkoa anasema mikakati ya kufungua kisiwa hicho inaendelea. Anasema ipo meli inayotengenezwa ambayo Juni mwakani itaanza safari zake kati ya Nyamisati, Wilaya ya Kibiti na Kilindoni (makao makuu ya Mafia). “Kukiwa na usafiri wa kuaminika, hata wawekezaji wataweza kwenda,” anasema Ndikilo. Anasema Mafia yenye fukwe za kuvutia ina kiwanja kizuri cha ndege na mazungumzo yanaendelea ili ndege za ATCL zifike kisiwani hapo. Anatoa mfano, inapofika msimu wa watalii wengi, ndege ndogo zinazokwenda kisiwani humo hujaa abiria jambo ambalo huwa vigumu kupata usafiri wa haraka wa anga. Kwa mujibu wa Ndikilo, zipo hoteli 15 za kitalii.“Mafia itakuja kufunguka,” anasema na kutaja uwepo wa fukwe nzuri kuwa ni fursa nyingine za kiuchumi ambayo hazijaanza kutumika kikamilifu. Ndikilo anasema maonesho na kongamano la fursa za uwekezaji ambalo maandalizi yake yanaendelea, linategemewa kuwezesha watu wengi kufahamu fursa za uwekezaji siyo tu kwa wilaya ya Mafia, bali Pwani nzima. Kampuni ya Magazeti ya Serikali (Tanzania Standard Newspapers - TSN) imesaini makubaliano ya pamoja na ofisi ya mkoa wa Pwani kusimamia maonesho yatakayoanza Oktoba Mosi hadi Oktoba 7. Malengo ya maonesho na kongamano ni kutanabaisha wana Pwani, Watanzania na dunia kwa ujumla kuhusu hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa viwanda. Ndikilo anasema wataonesha umma fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Pwani, si tu kwenye viwanda, bali pia katika kilimo, mifugo, uvuvi, utalii na huduma mbalimbali. Taarifa ya mkoa inaonesha Pwani ina viwanda 1,192 ambavyo kati yake, 56 ni vikubwa, 85 vya kati, 350 ni vidogo na vilivyobaki ni vidogo zaidi. Vinachangia ajira za moja kwa moja 30,000 na zisizo za moja kwa moja 60,000. Mkuu wa mkoa anakiri kwamba pamoja na idadi hiyo, mkoa haujafanya vizuri kwenye viwanda vya usindikaji wa mazao ya shambani na uwekezaji katika kilimo, ufugaji na uvuvi. “Tukihamasisha uwekezaji katika kilimo, tutakuwa na mchango mkubwa kwenye kupunguza umasikini,” anasema. Uanzishaji wa kiwanda cha nazi, uboreshaji wa usafiri katika wilaya ya Mafia kama anavyoeleza mkuu wa mkoa wa Pwani, ni hatua mwafaka ya kutatua changamoto ya wakulima kukosa masoko na kulazimika kuuza mazao yao kwa bei ya kutupa. Kiwanda cha Wamalaysia kinachotarajiwa kuanzishwa, kutaleta soko la mazao karibu na wakulima kwa maana ya kuuza nazi zao moja kwa moja kiwandani badala ya kusubiri wanunuzi. Usafiri wa uhakika, hususani wa meli, utarahisisha watu kuingia na kutoka jambo ambalo itakuwa fursa kwa wafanyabiashara kwenda kununua zao hilo na mengine kwa bei isiyoumiza mkulima. | 3 |
HOSPITALI ya Taifa Muhimbili -Mlonganzila jijini Dar es Salaam, imewahakikishia Watanzania kuwa huduma zinazotolewa hospitalini hapo, zimeboreshwa. Pia imesema wagonjwa wanaotibiwa hapo, wameongezeka katika makundi yote.Imesema wagonjwa wa nje, wameongezeka kutoka 17,115 katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba 2018 kufikia wagonjwa 25,493 katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2019 ambalo ni ongezeko la asilimia 48.8.Aidha, wagonjwa wanaotibiwa na kulazwa wameongezeka kutoka 1,459 katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba 2018 na kufikia wagonjwa 2,795 katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2019, ambalo ni ongezeko la asilimia 91.6. Aidha, wagonjwa wanaotibiwa na kulazwa wameongezeka kutoka 1,459 katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba 2018 na kufikia wagonjwa 2,795 katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2019, ambalo ni ongezeko la asilimia 91.6.Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, akitoa ufafanuzi tuhuma zinazosambaa mitandaoni kwamba wagonjwa wengi wanapoteza maisha katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila (MNH-Mloganzila).Profesa Museru alisema katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2019, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH - Upanga) ililaza wagonjwa 17,230 na kati ya hao vifo vilikua 1,673, ambayo ni asilimia 9.7.Alisema hivyo basi takwimu kati ya MHN-Mlongazila na MNH- Upanga za asilimia ya wagonjwa waliofariki dunia hazitofautiani sana, ambapo MNH-Upanga ni asilimia 9.7 wakati MNH-Mloganzila ni asilimia 10.4 katika robo ya Julai hadi Septemba, 2019.“Hatua hii inaonyesha juhudi ambazo zinafanyika za kuboresha utoaji wa huduma katika MNHMloganzila zinazaa matunda,” alisema.Kuhusu tuhuma kuwa madaktari wanaotoa huduma MNHMloganzila ni wanafunzi waliopo katika majaribio, alisema si za kweli, kwa kuwa hospitali hiyo ina madaktari bingwa 52, madaktari wa kawaida 50 na kwa sasa ina madaktari tarajali 53.“Licha ya madaktari bingwa hawa walioajiriwa MNH-Mloganzila kutoa huduma, lakini pia wanashirikiana na madaktari bingwa kutoka MNH-Upanga katika kutoa huduma hapa MNH-Mloganzila, vilevile hospitali hii ina madaktari wawili waliobobea wenye hadhi ya Profesa kutoka Korea, nao wapo wanatoa huduma,”alisema.Alisema madaktari ambao wapo mafunzoni, hawafanyi kazi bila usimamizi kwani hospitali imeweka utaratibu wa kila mgonjwa anayefika kupata huduma, kuonwa na daktari bingwa kwa ajili ya maamuzi.Alisema uongozi wa hospitali unafanyia kazi tuhuma na malalamiko yaliyotolewa juu ya utoaji huduma katika taarifa hiyo ya kwenye mitandao. Alieleza wananchi kwamba tangu MNH, ipewe dhamana ya kusimamia hospitali hiyo ya Mloganzila, uongozi umetatua changamoto zilizokuwepo katika utoaji huduma na kwa kiasi kikubwa kuna mafanikio, ambayo yanaonesha kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa na pia wagonjwa ambao wametibiwa, wameshuhudia na kuridhika na utoaji wa huduma zake.“Tunawahakikishia Watanzania kuwa huduma zinazotolewa na MNH-Mloganzila zimeboreshwa. Tunawakaribisha Watanzania wenye jukumu la kuelimisha jamii, waje kuzungumza na wataalam na waone jinsi huduma zinavyotolewa ili waweze kutoa taarifa sahihi kwa jamii” alisema Profesa Museru. | 3 |
Mwandishi wetu, Tanga WAFANYABIASHARA wa Mkoa wa Tanga, wamesema hawaoni shidakulipa kodi baada ya kuona utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleoinayofanywa na Rais Dk. John Magufuli kupitia kodi zao. Hayo yalizungumzwa na wafanyabiashara wakati wa kampeni ya elimukwa mlipakodi inayoendelea mkoani humo ambako maafisa wa Mamlakaya Mapato Tanzania (TRA) kutoka Makao Makuu kwa kukishirikiana namaafisa wa TRA mkoa wa Tanga. Maafisa hao waliwatembelea wafanyabiashara kwenye maduka yaoyaliyopo barabara za namba jijini Tanga kwa lengo la kuwaelimisha nakuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati.Sambamba na hilo, maafisa hao pia waliweza kusikiliza kerozinazowakabili wafanyabiashara mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusikiliza maoni yao kama mpango wa kutengeneza mazingira rafiki kati yao naTRA.Thabiti Salimu ambaye ni mfanyabiashara wa Ukwaju wa jumla na rejarejakatika eneo la barabara za namba amesema kuwa, atamshangaamfanyabiashara atayekwepa kulipa kodi hususani katika kipindi hikiambacho wameshuhudia miradi mingi ikitekelezwa kupitia kodi zao. “Rais Magufuli anatumia kodi zetu vizuri, tunaona utekelezaji wa miradimingi ya maendeleo hivyo lazima tuendelee kulipa kodi la sivyo kazi yautekelezaji wa miradi hii itakwama,” alisema Salimu. Naye Dina Mbenu, mfanyabiashara wa vipuli vya pikipiki amesema kuwa,ikiwa wafanyabiashara watakwepa kulipa kodi watasababisha madhara yakiuchumi na kuathiri jitihada za serikali za kuboresha miundombinuikiwemo barabara. Amesema hatua ya maafisa wa TRA kuwatembelea kwenye maduka yaokwa lengo la kuwahamasisha kulipa kodi na kusikiliza kero na maoni yaoinawasaidia kutopoteza muda kwenye ofisi za TRA wakisubiri kuhudumiwa. Kwa upande wake Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi Julius Mjenga amesemazoezi la kuwatembelea wafanyabiashara ni endelevu na kabla ya kufanyikaTanga, zoezi hilo limeshafanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza,Mbeya na Morogoro. Amesema lengo la kufanya hivyo ni kutoa elimu ya kodi, kuwakumbushawafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati, kusikiliza maoni yao pamoja nachangamoto kwa ajili ya kuzitatua.Naye Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure, aliwaombawafanyabiashara kuunga mkono zoezi linalofanywa na maafisa wa TRA lautoaji elimu ya kodi, kusikiliza maoni na changamoto zao kwa kuwa zoezi hilo linalenga kuboresha huduma kwa mlipakodi.“Niwaombe wafanyabiashara wote mkiwaona maafisa wanatembelea,msifunge maduka, wapokeeni na kuwapa ushirikiano kwa kuwa wanalengakuwaelimisha na kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili kwenyebiashara zenu ambazo kwa pamoja tunaweza kuzitafutia ufumbuzi,”alisema Owure. Amesema zoezi hilo la utoaji wa elimu ya kodi kwa wafanyabiasharamkoani humo linatarajiwa kumalizika Juni 30, 2020 na kwamba lengo likiwani kutaka kuwafikia wafanyabiashara wengi mkoani hapo. | 5 |
Na WINFRIDA NGONYANI-DAR ES SALAAM MWANARIADHA wa Tanzania aliyeibuka shujaa kwa kushika nafasi ya tano katika mbio ndefu (marathon) kwenye michezo ya Olimpiki mwaka huu, Alphonce Simbu, ameitaka Serikali kuanza mara moja harakati za kusaka medali mwaka 2020 michezo hiyo itakapofanyika jijini Tokyo, Japan. Simbu alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, akitokea jijini Rio de Jeneiro, nchini Brazil alikokwenda kushiriki michezo ya Olimpiki. Alisema asilimia kubwa ya wanamichezo waliofanya vizuri katika michezo ya Olimpiki mwaka huu waliandaliwa vyema na nchi zao tofauti na ilivyokuwa kwa upande wake. “Wenzetu waliandaliwa vyema, mimi naamini uwezo wa Tanzania kupata medali ya dhahabu kwenye michezo ya Olimpiki upo, lakini endapo Serikali itaanza kampeni ya kutimiza lengo hilo kuanzia sasa na si kusubiri michezo inapokaribia,” alisema Simbu. Aidha, Simbu aliongeza kwamba haikuwa kazi rahisi kwake kushika nafasi ya tano kama watu wanavyodhani kwa kile alichodai kuwa akiwa katika mbio ndefu ‘marathon’ alichuana vikali na wanariadha mashuhuri na wakongwe waliokuwa na uchu wa kupata medali. “Changamoto ambayo sitaweza kuisahau ni pale nilipofika umbali wa km 20 nikiwa karibu kabisa na Mkenya, Kipchoge Eliud (mshindi wa mbio hizo) kwa kweli hapo ndipo niliona mbio ni ngumu. “Kipchoge alikuwa anakimbia mwendo kasi ajabu na endapo ningefuata nyayo zake hakika nisingefika popote na badala yake ningeishia kuwa mtu wa mwisho kabisa. Lakini niliamua kwenda na kasi niliyoanza nayo na hatimaye kuwapita wenzangu zaidi ya 100,” alisema. Mwanariadha huyo kijana aliyeshiriki michezo ya Olimpiki kwa mara ya kwanza, alikimbia mbio za marathon akitumia muda wa saa 2:11:15, ambapo aliwashukuru Watanzania, Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) na Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) kwa sapoti waliyompa kufanikisha ushindi wake. Naye Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi, alisema kamati hiyo kwa kushirikiana na RT itaandaa mpango mkakati kuhakikisha wanariadha wengi zaidi wanashiriki mbio za kimataifa zikiwamo ya Nyika na zile za dunia zitakazofanyika mwakani kama sehemu ya maandalizi ya Olimpiki ya mwaka 2020. Kwa upande wake mwanariadha mkongwe, Juma Ikangaa ambaye aliwahi kushika nafasi ya sita mwaka 1984 na nafasi ya saba mwaka 1988 katika michezo ya Olimpiki iliyofanyika jijini Soul, Korea, aliwataka Watanzania kuacha kubeza ushindi wa Simbu. Shujaa huyo aliwasili nchini saa 9 alasiri akiambatana na wanariadha wenzake ambao ni Saidi Makula aliyeshika nafasi ya 43 na Fabiano Joseph aliyemaliza nafasi ya 112. | 4 |
NA MICHAEL MAURUS, ZANZIBAR KOCHA msaidizi wa Simba, Mganda Jackson Mayanja, amesema kuwa amekuja katika timu hiyo ili kurejesha soka lao la asili ambalo ni la kitabuni la pasi fupi fupi na za haraka, lakini pia kuwawezesha wachezaji kuwa na stamina ya kutosha pamoja na umakini wa hali ya juu. Wachezaji wa Simba jana walionja joto ya jiwe, baada ya kuhenyeshwa na kocha huyo kwa kufanya mazoezi kwa dakika 140 kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani hapa. Akizungumza na MTANZANIA jana, Mayanja alisema Simba ina soka lake la asili ambalo kwa kipindi halijaonekana, hivyo uwepo wake katika klabu hiyo utasaidia kulirudisha. “Simba ni timu kubwa ambayo ina utamaduni wake, nafahamu aina ya soka la Simba, ni soka la kuvutia. Niko hapa kuifanya kazi yangu kama ambavyo viongozi wa Simba wanategemea na ninawaahidi watu wa Simba sitawaangusha,” alisema. Alisema iwapo aliweza kuifanya Kagera Sugar kuwa tishio enzi hizo, basi itakuwa ni zaidi kwa Simba iliyosheheni wachezaji wenye uwezo mkubwa, lakini ikiwa ni timu kubwa yenye kila aina ya nyenzo za kumwezesha kufanya kazi yake ipasavyo. “Lakini ili niweze kufanikiwa katika hayo, nimelazimika kuanza na kuwajenga kisaikolojia wachezaji, lakini pia kurejesha morari na kila mmoja kufahamu thamani yake ya kuwa katika timu kubwa kama Simba,” alisema. Mayanja jana alianza mazoezi yake saa 10:15 asubuhi na kumaliza saa 12:35 mchana, huku akiwatoa jasho nyota wa timu hiyo. Katika mazoezi yake hayo, Mayanja alianza kwa kuwajengea wachezaji wake stamina kupitia mazoezi ya viungo yaliyodumu kwa dakika 15 kabla ya kuhamia katika kuchezea mpira. Akizungumzia mazoezi ya kocha huyo, Nahodha wa Simba, Hassan Isihaka, alisema wameyafurahia akiamini yanaweza kuwasaidia kufanya vema kwenye mechi zao zijazo za Ligi Kuu Tanzania Bara. Alisema kocha huyo anaonekana kuwa makini zaidi na kazi yake, akiahidi wachezaji wote kumpa ushirikiano unaostahili ili aweze kutimiza malengo yake. “Tumempokea vizuri kocha wetu mpya na tunaahidi kumpa ushirikiano pamoja na kufuata maelekezo yake,” alisema Isihaka ambaye ni beki wa kati wa kutumainiwa wa Simba. Kikosi cha Simba kilichokuwa kimeweka kambi visiwani hapa tangu ilipotolewa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi ambayo fainali yake ilitarajiwa kufanyika jana kati ya Mtibwa Sugar na URA ya Uganda, inarejea Dar es Salaam leo jioni kuendelea na kambi yake. Wachezaji wote wa timu hiyo walikuwapo kambini kasoro Abdi Banda, ambaye inadaiwa alirejea Dar es Salaam kwa ajili ya kufanyiwa vipimo kutokana na majeraha ya paja yaliyokuwa yakimkabili tangu wiki iliyopita, kwa mujibu wa daktari wa Simba, Gembe. | 4 |
Miongoni mwa vifaa hivyo ni mashine ya kukaushia nywele, vifaa vya kuoshea nywele, viti na masinki. Vitendea kazi hivyo mbalimbali vitamuwezesha kupanua wigo wa huduma zinazopatikana katika saluni yake.Akikabidhi vifaa hivyo Meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel , Hawa Bayumi alisema sambamba na kuongeza idadi ya huduma zitakazopatikana katika saluni ya Prisca, vifaa hivyo vitamuwezesha kuhudumia wateja wengi zaidi kwa wakati mmoja.Alisema hali hiyo itamuwezesha Prisca kuajiri vijana wenziwe ili kuendeleza biashara na kukuza kipato chake.Bayumi alisema mpango huo wa kuwawezesha wajasiriamali vijana ili kuwaongezea kasi ya maendeleo ya kibiashara ni sehemu ya kurudisha mapato ya kampuni hiyo kwa jamii kwa namna inayoleta tija kwa taifa.“Sisi tumeona ni vizuri kushirikiana na wajasiriamali na hasa vijana ili kuhakikisha tunawawezesha na kukuza mitaji yao ya biashara kwa mafunzo na vifaa,” alisema meneja huyo.Awali akipokea msaada huo Prisca ameshukuru kwa vifaa hivyo na kuahidi kuendeleza zaidi biashara hiyo ili kutimiza ndoto zake za kuwa mfanyabiashara mkubwa.“Naahidi kuongeza juhudi na kutumia vyema msaada huu ili kuhakikisha nakuza na kuendeleza biashara yangu lakini pia nitatoa fursa kwa vijana wenzangu,” alisema Prisca. Kampuni ya simu ya Airtel inazunguka nchi nzima kukutana na vijana kwa lengo la kuwapa elimu ya ujasiriamali. | 5 |
NA JUDITH PETER, DAR ES SALAAM TIMU ya Simba imerudisha matumaini ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani baada ya kuwachapa wapinzani wao, Azam FC mabao 2-1 mchezo uliofanyika jana Uwanja wa Taifa jijini hapa. Simba na Azam zipo kwenye vita kali ya kuwania nafasi ya pili ili kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho mwakani, ambapo wekundu hao wameshindwa kukata tiketi ya michuano ya kimataifa toka mwaka juzi waliposhiriki mara ya mwisho. Azam ambayo mara baada ya mchezo huo imebakiwa na pointi 45 ikiwa na mechi mbili mkononi dhidi ya Yanga keshokutwa na Mgambo JKT Jumamosi hii, inahitaji pointi tatu tu kwenye mechi hizo zitakazoifanya kufikisha pointi 48 ambazo hazitaweza kufikiwa na Simba. Simba yenye pointi 44 inabidi iiombee mabaya Azam ipate sare mechi hizo au ifungwe zote, huku na yenyewe ikitakiwa kuifunga JKT Ruvu kwenye mchezo wa mwisho Jumamosi hii ili kupata tiketi ya michuano hiyo. Wekundu hao walianza kwa kasi mchezo huo na kufanya kosakosa langoni mwa Azam kupitia kiungo, Said Ndemla dakika ya 12 aliyepiga shuti kali la mbali ambalo lilidakwa vema na kipa Aishi Manula. Azam waliamka dakika ya 14 na kufanya shambulizi kali langoni mwa Simba kupitia kwa Kipre Tchetche, lakini Didier Kavumbagu anakosa bao la wazi akiwa na kipa Ivo Mapunda, baada ya kupiga shuti hafifu lililodakwa kirahisi. Dakika ya 37, mwamuzi wa kati, Israel Nkongo wa jijini hapa alimuonya kwa kadi ya njano kiungo wa Azam, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ kwa kumchezea madhambi kiungo wa Simba, Jonas Mkude. Azam ilipata pigo dakika mbili baadaye baada ya Sure Boy kupewa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumfanyia madhambi beki Mohamed Hussein na hivyo kulazimika kucheza pungufu hadi mwisho wa mchezo. Kabla ya timu zote kwenda mapumziko, ilitokea piga nikupige langoni mwa Simba baada ya kiungo wa Azam, Frank Domayo kuingiza krosi iliyowababatiza mabeki wa Simba na Mapunda alilazimika kufanya kazi ya ziada kuokoa na kufanya kipindi cha kwanza kuisha kwa suluhu. Azam ilifanya mabadiliko kipindi cha pili kwa kumtoa Domayo na kuingia Bryson Rafael, kisha ikamtoa beki Pascal Serge Wawa na kuingia kiungo Mudathir Yahya. Simba ilitumia vema mwanya wa Azam kuwa pungufu kwa kupata bao la uongozi dakika ya 48 lililofungwa na mshambuliaji Ibrahim Ajibu akiunganisha vema pasi ya beki Hassan Kessy. Dakika ya 53, Azam ilijibu mapigo kwa kusawazisha kupitia kwa Mudathir aliyeingia kipindi cha pili, kiungo huyo alipokea pasi ya Tchetche na kupiga shuti akiwa ndani ya eneo la 18 lililomshinda kipa wa Simba. Azam iliyovuliwa ubingwa wa ligi na mabingwa wapya Yanga Jumatatu iliyopita, ilifanya mabadiliko dakika ya 67 kwa kutoka Kavumbagu na kuingia nahodha John Bocco aliyetoka kwenye majeruhi. Simba ilimaliza mchezo huo dakika ya 74 kwa kupata bao la pili lililofungwa na Ramadhan Singano ‘Messi’ baada ya kupiga krosi iliyodunda chini na kutinga wavuni moja kwa moja, Messi alifunga akitumia vema pande la Mkude. Mwamuzi alilazimika kumwonyesha kadi ya njano Messi baada ya kushangilia bao hilo kwa kuvua jezi yake. Licha ya dakika saba kuongezwa kufuatia dakika 90 kumalizika, Simba ilimaliza mpira huo kwa ushindi huo. Oscar Assenga kutoka Uwanja wa Mkwakwani, Tanga naye anaripoti kuwa, wenyeji Coastal Union wamefanikiwa kujiondoa kwenye janga la kushuka daraja baada ya kuichapa Stand United mabao 3-1 na kufikisha pointi 31. Mabao ya Coastal yaliyoiweka kwenye hali mbaya Stand yamefungwa na Ayoub Semtawa dakika ya 17, Yusuph Chuma (dk 42) na Mnigeria, Bright Obina (dk 69), huku lile la Stand likifungwa na Mnigeria, Chidiebere Abisirim. Kutoka kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro wenyeji Mtibwa Sugar wameilaza Ruvu Shooting mabao 2-0 na kuiweka pabaya zaidi timu hiyo ya jeshi kwenye janga la kushuka daraja ikiwa na pointi 29. | 4 |
SERIKALI imeombwa kuweka udhibiti wa uingizaji wa vigae kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kulinda soko la viwanda vya ndani. Ombi hilo lilitolewa juzi na Meneja Biashara na Uhusiano wa kampuni ya Good Will, Msafiri Figa, inayoendesha kiwanda kinachozalisha vigae Will kilichopo wilayani Mkuranga katika Mkoa wa Pwani. Akizungumza na timu ya waandishi wa habari wa kampuni ya magazeti ya serikali ya Tanzania Standard Newspaper (TSN), alisema kiwanda chao kinaathirika kimasoko kutokana na uwapo wa bidhaa hizo za nje ambazo hazina tofauti na wanazozalisha wao. Aliwaambia waandishi hao walioweka kambi na kuandika habari za Pwani kuelekea maonesho ya viwanda na kongamano la uwekezaji litakalofanyika wiki ijayo kwamba, walipoanza uzalishaji Aprili mwaka juzi, walitarajia soko la ndani litakuwa asilimia 70 na iliyobaki ni la nje lakini imekuwa kinyume. “Ukiacha ushindani wa viwanda vingine vya hapa nchini vinavyozalisha vigae, ambayo hiyo hatuna shida nayo, changamoto kubwa iliyopo ni uingizaji wa tiles (vigae) kutoka nje ya nchi. Tunaomba serikali iliangalie suala hili,” alisema Figa.Alisema takribani boksi 10,000 za vigae zipo ghalani kiwandani hapo kwa kukosa soko kutokana na kuingiliwa kwa bidhaa hiyo ya nje. Alishauri serikali kuweka udhibiti kwa kuongeza kodi au kuweka masharti yanayotaka vigae vinavyoingizwa nchini viwe ni aina ambayo haizalishwi nchini. Alisema katika kukabili changamoto ya masoko, wameamua kufungua ghala jijini Dar es Salaam ambako wanauza wenyewe bidhaa tofauti na awali walipotumia mawakala. Vile vile wanakwenda mikoani sambamba na kutoa ruhusa kwa wateja kununulia kiwandani vidhaa zao, jambo ambalo awali halikufanyika. Hata hivyo, alishukuru agizo la serikali la kutaka taasisi zake kuhakikisha zinanunua bidhaa za nchini katika miradi mbalimbali akisema limeleta manufaa kwao kutokana na halmashauri nyingi kununua vigae wanavyozalisha. Changamoto nyingine aliyoomba serikali kuifanyia kazi, ni kurekebisha bei ya gesi aliyosema iko juu. Kwa mujibu wa meneja huyo, umeme unaotumika kuendesha kiwanda hicho ni wa gesi na kwa mwezi wanatumia mamilioni ya shilingi kuinunua. | 3 |
Stars inayofundishwa na Charles Boniface Mkwasa, inaingia uwanjani ikiwa inajivunia ushindi wa mabao 2-0 iliyoupata katika mechi ya kwanza Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kikosi cha Stars kinachodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kiliwasili salama katika mji wa Blantyre juzi jioni tayari kwa mchezo wa leo.Stars iliondoka Dar es Salaam juzi alfajiri kwa usafiri wa shirika la ndege la Fastjet na kuwasili katika Jiji la Lilongwe saa 4 asubuhi kabla ya kuanza safari ya basi kwenda Blantyre iliyochukua takribani saa tatu.Kwa mujibu wa taarifa kutoka Blantyre, wachezaji wote wapo katika hali nzuri, na Stars ilitarajiwa kufanya mazoezi jana jioni kwenye Uwanja wa Kamuzu Banda ambao utatumika kwa mchezo wa leo.Kocha Mkuu Mkwasa anayesaidiana na Hemedi Morocco, alisema vijana wake wote wapo katika hali nzuri kiafya, kifikra na morali ni ya hali ya juu kuelekea kwenye mchezo huo.Mkwasa na msaidizi wake hawatarajiwi kubadilisha kikosi kilichoanza Jumatano dhidi ya Malawi kwa kuanza na Ally Mustapha, Shomari Kapombe, Mwinyi Haji, Kelvin Yondani, Nadir Haroub, Himid Mao, Thomas Ulimwengu, Said Ndemla, Mbwana Samatta, Mrisho Ngassa na Farid Mussa.Katika hatua nyingine, mabasi mawili yenye mashabiki wa Stars yalitarajiwa kufika jana mjini Blantyre tayari kuipa nguvu timu hiyo ambayo ikitoa Malawi itacheza na Algeria katika hatua ya pili ya kufuzu kwenda Urusi 2018.Wakati huo huo, Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerry amesema kama Taifa Stars inahitaji kusonga mbele leo dhidi ya Malawi itafute mabao ya mapema ili kuwapunguza presha.Akizungumza na gazeti hili jana kwenye fukwe za Kunduchi, Dar es Salaam, Kerry alisema Taifa Stars wana nafasi ya kusonga mbele kama tu watashambulia dakika 20 za kwanza na kufunga ndipo watafanikiwa.“Naamini Taifa Stars wana nafasi ya kufanya vizuri ingawa naona kama mchezo unaweza kuwa mgumu kwa sababu Malawi ni timu nzuri na ilionesha mchezo safi ule wa awali,” alisema kocha huyo Mwingereza. Kerry alisema Taifa Stars wana nafasi ya kushinda kwani wao pia wana kikosi kizuri ambacho kama kitazingatia maelekezo wanayopewa kitafika mbali. | 4 |
['Meneja wa Tottenham, Mauricio Pochettino, anasema kuwa anahofia kufutwa kazi kutokana na matokeo mabaya ya klabu hiyo (Mirror)', 'Juventus na Atletico Madrid zinamfuatilia beki wa West Brom wa miaka 19, Nathan Ferguson.(Sun)', 'Mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Olivier Giroud, 33, anatakiwa na Crystal Palace na huenda akajiunga na klabu hiyo ifikapo mwezi Januari. (Daily Star)', 'Real Madrid haitajaribu kumsaini mchezaji wa safu ya kati wa Tottenham raia wa Denmark, Christian Eriksen, 27, mwezi Januari hadi watakapowauza wachezaji wasiokuwa katika kikosi cha kwanza. (AS)', 'Real itaipatia Spurs kiungo wao wa kati wa Uhispania Isco, 27, na mshambuliaji wa Jamuhuri ya Dominica Mariano Diaz, 26, katika juhudi ya kupata saini ya Eriksen. (El Desmarque - in Spanish)', 'Mshambuliaji wa Chelsea na England Tammy Abraham, 22, anakaribia kutia saini mkataba mpya wa kusalia Stamford Bridge baada ya kufunga mabao manane katika ligi ya Premia msimu huu. (Daily Star)', 'Barcelona imemaliza mzozo wake na Atletico Madrid kuhusu usajili wa Antoine Griezmann, 28, kwa kumlipia euro milioni 15 zaidi mshambuliaji huyo wa Ufaransa. (El Mundo - in Spanish)', 'Derby itampatia nahodha wa zamani wa England Wayne Rooney, 33, mafunzo maalum kuhakikisha yuko tayari kwa mashindano atakapojiunga na klabu hiyo kutoka DC United. (Mail)', 'Kiungo wa kati wa Brazil na Manchester United Fred, 26 - ambaye alinunuliwa kwa kima cha £47m kutoka Shakhtar Donetsk mwezi Juni 2018 - anaamini kuwa ameanza kupata uzoefu wa soka la Uingereza. (Telegraph) ', "Arsenal inaongoza katika kinyang'anyiro cha usajili wa beki wa RB Leipzig na Ufaransa wa chini ya miaka-21 Dayot Upamecano, 20, ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa euro milioni 50. (Mail)", 'Meneja wa Italia Roberto Mancini huenda akamjumuisha kipa mkongwe wa Juventus Gianluigi Buffon, 41, na kiungo wa kati wa Boca Juniors wa miaka 36 Daniele de Rossi katika kikosi cha Euro 2020. (Rai Sport via Mail)', 'Meneja wa Real Madrid, Zinedine Zidane amesema anataka kusalia klabu hiyo maisha. (Marca)', 'Beki wa zamani wa Arsenal na England Sol Campbell, 45, anafanya mazungumzo ya kuwa mkufunzi wa Southend, inayoshiriki soka la daraja ya kwanza - miezi miwili baada ya Macclesfield inayocheza soka ya daraja la pili. (Sun)', 'Real Madrid inawafuatilia winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 19 na mshambuliaji wa Norway wa miaka 19- Erling Braut Haaland, anayechezea Red Bull Salzburg. (El Desmarque, via Mail)', 'Meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anataka kumsajili mshambuliaji wa Ujerumani na RB Leipzig Timo Werner,23 ambaye aliwahi kuhusishwa na tetesi za kujiunga na Liverpool. (Express)', 'Manchester United pia inajiandaa kumpatia mkataba mpya kiungo wa kati wa Uingereza Angel Gomes, 19, licha ya tetesi kuwa Barcelona inamtaka. (Sun)', 'Meneja wa Chelsea Frank Lampard anataka mshamsmbuliaji wa Ufaransa wa miaka 33, Olivier Giroud, ambaye hajafurahishwa na hatua ya kutojumuishwa katika kikosi cha kwanza aendelee kusalia Stamford Bridge. (Telegraph)', 'Chelsea imemuongeza mchezaji wa safu ya kati wa Atalanta na Ukraine Ruslan Malinovskyi, 26, katika orodha ya wachezaji amabao huenda wakahamia klabu hiyo msimu ujao wa joto. (Express) '] | 4 |
NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm, amesema kurejea kikosini kwa kiungo, Haruna Niyonzima, ni jambo la furaha kwani timu hiyo inahitaji mchezaji wa aina yake mwenye uwezo wa kuwatetemesha wapinzani. Ijumaa ya wiki iliyopita uongozi wa klabu ya Yanga ulimaliza tofauti zilizokuwepo kati yake na Niyonzima na juzi aliingia rasmi uwanjani kucheza dhidi ya Friends Rangers katika mchezo wa Kombe la FA. Katika mchezo huo uliopigwa juzi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga walishinda mabao 3-0 na kufanikiwa kutinga hatua ya 16 ya Kombe la FA ili kuwania tiketi ya kufuzu kucheza Kombe la Shirikisho mwaka 2017. Akizungumza Dar es Salaam juzi, Pluijm alisema si kwamba katika kikosi chake hakuna wachezaji wazuri bali uwezo na sifa alizonazo kiungo huyo ni muhimu kwa timu hiyo. Akizungumzia mchezo wa juzi, Pluijm alisema hakupata tabu ya kuwafunga wapinzani wao kwa kuwa anawafahamu vizuri kwani walishakutana mara mbili kwenye mechi za kirafiki. “Niliwasoma vizuri kwenye mechi mbili tulizocheza, hivyo ilikuwa ni kazi rahisi kuwakabili na kuhakikisha tunapata mabao ya mapema kwani ndiyo njia inayoweza kuwatoa mchezoni na kutupa nafasi ya kufunga zaidi,” alisema. Alisema nyota sita wa kikosi hicho walikuwa wakisumbuliwa na majeraha, lakini aliowapa nafasi walionyesha uwezo mkubwa na kufanikiwa kuipa timu ushindi ingawa wangeweza kufunga mabao mengi zaidi. | 4 |
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40) na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu. | 5 |
Na MWANDISHI WETU-SINGIDA WANANCHI wa Kata ya Kinampanda, Wilaya ya Iramba mkoani Singida, wataondokana na kero ya huduma bora za afya baada ya ujenzi wa kituo cha afya katika kata hiyo kukamilika. Hayo yalisemwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (CCM), alipozungumza na wananchi wa kata hiyo jana. Alisema kwamba, mkandarasi wa ujenzi huo ameshapatikana na Jumatatu ijayo ataanza kazi na kwamba wanatarajia ifikapo mwakani kituo hicho kianze kufanya kazi. Waziri huyo aliahidi kutoa mifuko 300 ya saruji na nondo 100 za kuanzia, huku akiwataka vijana wajitolee kufyatua matofali. “Kinampanda ndio ‘centre’ kubwa ya watu wanaotoka maeneo mbalimbali, huduma ikiwa nzuri mtu ataanzia hapa kabla ya kufika Kiomboi. “Tuna vijiji ambavyo vimezuiwa na mto kwenda Kiomboi, hapa Kinampanda ni karibu zaidi hivyo tuunge mkono ujenzi huu,” alisema Mwigulu. Alisema kituo hicho kitakuwa na hadhi na ukubwa wa kutosha ambapo kitakuwa na sehemu ya matibabu ya kawaida, kulaza wajawazito na kulaza wagonjwa wengine. Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Kinampanda, Samwe Kiula, alimshukuru mbunge huyo kwa kuleta ujenzi huo na kuwataka wananchi kuwa tayari kuchangia baadhi ya vitu vitakavyokuwa vinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo. Kwa upande wao vijana wa Iramba wakiwakilishwa na Katibu wa Vijana CCM, Abel Makala, walisema wako tayari kuweka kambi sehemu kunapofanyika ujenzi huo ili kuunga mkono juhudi za ujenzi huo. | 3 |
KAHAWA ya Uganda imepata bahati ya kupigiwa chapuo katika soko kubwa lenye watumiaji wengi wa kahawa nchini Urusi.Baada ya kufanya vizuri katika masoko ya nchi za Ulaya Magharibi kwa muda mrefu, Uganda imeanza kutangaza kahawa yake katika nchi za Ulaya Mashariki na sasa iko katika soko kubwa duniani la kahawa nchini Urusi.Kwa mujibu wa taasisi ya uzalishaji wa kahawa nchini Urusi (Rusteacoffee), soko la kahawa nchini humo lina thamani ya Dola za Marekani milioni 750. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na taasisi hiyo kubwa ya kahawa katika nchi hiyo, thamani ya soko la kahawa kwa sasa imepanda hadi kufikia Dola za Marekani bilioni 2.5. Takwimu hizo zimeonesha kuwa, kila mwananchi wa Urusi anaweza kutumia kahawa kilo 1.7.Kiwango hicho ni kikubwa ikilinganishwa na idadi ya wananchi wa nchi hiyo. Kwa hali hiyo, ina maana kila mwananchi wa nchi hiyo anakunywa vikombe vya kahawa 120 kwa mwaka.Hii inaonesha Urusi ni soko kubwa na muhimu kwa biashara ya kahawa ya Uganda. Katika kuhakikisha kuwa kahawa ya Uganda inatangazwa vya kutosha katika soko la kahawa nchini Urusi, Mamlaka ya Ustawishaji wa Kahawa Uganda (UCDA) imeungana na ubalozi wa nchi hiyo mjini Moscow katika maonesho ya aina mbalimbali za kahawa na chai yaliyofanyika katikati ya mwezi uliopita.Uganda ni moja ya mataifa ya Afrika Mashariki yanayozalisha kahawa kwa wingi na imefanikiwa kuwa na kahawa yenye ubora wa hali ya juu. Ubora huo umechangia kwa kiasi kikubwa kukubalika kimataifa na kujipatia masoko katika mataifa mengi duniani. Mataifa mengine ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayozalisha kahawa kwa wingi ni Tanzania, Kenya na Rwanda. | 3 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.