text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
Mbali na kutowasikiliza makocha, mwanariadha Failuna Abdi alionesha utovu mkubwa wa nidhamu timu hiyo ilipokuwa ikirejea nchini kwenye Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere mbele ya viongozi wa Riadha Tanzania (RT) pamoja na wale wa Kamati ya Olimpiki (TOC) baada ya kugoma kwenda kambini Kibaha na kutokomea kusikojulikana bila kuaga.Kwa mujibu wa taarifa ya Kocha Mkuu wa timu ya riadha iliyoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, Zakarie Barie, baadhi ya wachezaji walionesha utovu wa nidhamu kambini kwa kuwabishia makocha kwa kugomea kumaliza programu za mazoezi.Barie akizungumza kwa njia ya simu alikiri kutokea kwa vitendo hivyo vya utovu wa nidhamu na kusema kuwa ameshatoa mapendekezo kwa wahusika, ambao kama wataona inafaa watawaadhibu wahusika ili iwe fundisho kwa wengine.Sehemu ya taarifa hiyo inasema: “Tabia hiyo mbaya ya kukosa nidhamu iliendelea tulipofika Dar es Salaam Airport wakati tuliporudi kutoka Australia, wakati katibu mkuu wa TOC alipokuwa akitoa mwongozo na utaratibu wa malazi na usafiri mwanariadha Failuna Abdi alionesha dharau kubwa mbele ya Katibu Mkuu wa TOC alipokataa kufuatana na wachezaji wengine na kuondoka bila kuaga. Hiyo ni dharau na kukosa nidhamu mbele ya kocha hata kwa wachezaji wenzake. Bila shaka katibu wa RT atalishughulikia na kukomesha tabia hiyo isiendelee tena.”Mbali na Failuna, mwanariadha mwingine Agustino Sulle jina lake lilienguliwa kutoka katika orodha ya wachezaji waliokwenda Australia baada ya kushindwa kuripoti katika kambi hiyo kwa madai ya kufanya hivyo baada ya kuambiwa na kocha wake, Thomas John.John pia ndiye kocha wa Failuna na Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday jana aliliambia Habari Leo kuwa kocha huyo naye anahusika moja kwa moja kwa Sulle kukacha kambi ya taifa, hivyo naye ana adhabu yake.Gidabuday alisisitiza kuwa wachezaji hao pamoja na Sarah Ramadhani ambaye alishiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, naye anahusika kwa vitendo vya utovu wa nidhamu wakati wa kambi hiyo mjini Arusha hivi karibuni ingawa hakutajwa katika ripoti ya kocha Barie.Taarifa zingine ambazo hazitathibitishwa zilisema kuwa baadhi ya wachezaji mbali na kuwa wajeuri kwa makocha, pia walikuwa wakimdharau matroni Lwiza John, huku wengine wakigoma kulala kambini na kulala kusikojulikana.Kamati ya Ufundi ya RT ilikutana Jijini Dar es Salaam juzi na kuzungumzia matokeo ya Jumuiya ya Madola pamoja na ripoti ya kocha Barie kuhusu utovu huo wa nidhamu, ambapo mapendekezo na maamuzi yamepelekwa kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Dk Singo Yussuph kwa utekelezaji.Naye Mkurugenzi wa Michezo, ambaye alikuwa mkuu wa msafara wa timu ya Tanzania iliyoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola, Dk Yussuph Singo alisema kuwa waliporudi ilikuwa wiki ya bajeti, hivyo walishindwa kukutana na kufanya tathmini.Alisema kwa sasa yuko Dodoma na anasubiri apate ripoti za michezo yote na ndio atalizungumzia hilo kwa ujumla na kujua siku watakayofanya tathmini, kwani kwa sasa hata ripoti ya RT haiajaipata. Mbali na riadha, Tanzania katika michezo hiyo ya Jumuiya ya Madola ilipeleka pia timu za ngumi, mpira wa meza pamoja na kuogelea.
4
MBUNGE wa Makambako, Deo Sanga maarufu Jah People (CCM), ameshauri Rais John Magufuli kuongezewa kipindi kimoja cha uongozi ambacho badala ya kumaliza urais mwaka 2025, akae hadi mwaka 2030.“Rais wetu (Magufuli) ana maono makubwa ya kuifikisha mbali nchi yetu, hivyo aombewe awe rais wa kudumu, aongezewe kipindi kimoja hadi mwaka 2030, “Mimi na wenzangu tutatembea nchi nzima kumuombea…ikifika mwaka 2021 wabunge tuanze kutembea nchi nzima kumuombea Rais Magufuli aongezewe muda,” alisema Sanga.Mbunge huyo aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, alitoa maoni yake hayo wakati akichangia Mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2019/2020 yaliyowasilishwa juzi na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.Naye Mbunge wa Kijitoupele, Shamsi Vuai Nahodha (CCM) alisema Rais Magufuli ana maono ya kulipeleka Taifa mbali zaidi na kuachana na kupitisha bakuli kwa wafadhili kuombaomba, hivyo kuwataka Watanzania kufanya kazi kwa bidii ili Taifa lijitosheleze. Kwa upande wake, Mbunge wa Kilombero, Peter Lijuakali (Chadema)alisema “Inasikitisha wabunge wana mawazo ya kutaka Katiba ifanyiwe marekebisho makubwa ili rais aongezewe muda…inafedhehesha sana.”Hata hivyo, Rais Magufuli mara kadhaa ameshasema hana mpango wa kuongeza muda wa uongozi na ikifika muda wake wa kuachia madaraka, atafanya hivo tarehe hiyohiyo anayotakiwa kufanya hivyo. Mbunge wa Moshi Mjini, Jaffar Michael (Chadema) alitaka wafanyabiashara wa masoko kutopewa vitambulisho vya ujasiriamali kwani kumesababisha halmashauri kukosa mapato na kushindwa hata kulipia gharama za kusafisha masoko hayo.Mbunge wa Kuteuliwa, Abdallah Bulembo (CCM), alitaka Wizara ya Madini na Tume ya Madini kuwasimamia watendaji wao wanaowanyima leseni wachimbaji madini walio safi, wasio na matatizo na wanaotaka kulipa kodi. Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Jaku Hashim Ayoub (CCM) aliitaka serikali kuwapeleka Zanzibar viongozi mashuhuri wanaotoka nje ya nchi wanaotembelea Tanzania.
3
Na JOHANES RESPICHIUS STAA wa Bongo anayetesa kwenye filamu, Kajala Masanja amevunja ukimya na kufunguka kuhusu maneno yanayozagaa mitaani yakimtaja kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa nyakati tofauti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Msamy Baby. Kwa muda mrefu sasa, minong’ono hiyo imekuwa ikizagaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii tangu wakati Makonda akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni katika Serikali iliyopita ya Dk. Jakaya Kikwete. Tetesi za uhusiano wake na RC Makonda, zilianza wakati Makonda (alipokuwa DC wa Kinondoni) akishirikiana na msanii huyo kwenye shindano la kusaka vipaji vya wasanii wa Wilaya ya Kinondoni lililojulikana kama Kinondoni Star Search. Katika mahojiano na Polisi wa Swaggaz, Kajala alipoulizwa kuhusu madai ya kuwa na uhusiano na Makonda, alijibu kwa kifu sana: “Hapana sijawahi kutoka naye kabisa. Hilo halipo.” Awali, RC Makonda aliwahi kuzungumzia madai hayo akiwa bado Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, ambapo alisema wabaya wake wa kisiasa wamekuwa wakisaka mbinu za kumchafua kila kukicha. Makonda, alikwenda mbali zaidi akisema kuwa, propaganda ya kumchafua ilianza tangu wakati wa Bunge Maalum la Katiba, alipokwenda Bungeni na msanii mwingine wa filamu, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, akazushiwa kuwa alitoka naye. Katika maelezo ya Makonda, alisema anawashangaa wengi wanavyomhusisha kuwa na uhusiano usiofaa na Kajala kwa vile ameshirikiana naye kwenye project hiyo ya kusaka vipaji wakati pia ameshirikiana na wasanii wengi wa kiume. Kwa Kajala inakuwa mara ya kwanza kuzungumzia hilo katika mahojiano maalum na mwandishi wa Swaggaz. Kuhusu msanii wa Bongo Fleva, Msami Baby Kajala alisema: “Hata huyo sijawahi kutembea naye, lakini nakiri kwamba ni rafiki yangu wa karibu kama msanii mwenzangu ila hatujawahi kuwa wapenzi hata siku moja.” SWAGGAZ: Vipi kuhusu picha zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii zikiwaonesha wewe na Msami mkiwa sehemu mbalimbali za starehe? KAJALA: Kwahiyo nikipiga picha na msanii basi natoka naye?  Mtu unaweza kujisikia kupiga picha na yeyote kwa ajili ya kurusha Insta, kwahiyo ukifanya hivyo tu basi tayari unatoka naye? Mfano leo (juzi Jumatano) nimepiga picha na Petty Man, kwahiyo nikiweka Insta basi itakuwa Kajala anatoka na Petty. Siyo jambo zuri, nadhani wangekuwa na uhakika kwanza, mimi sijawahi kutembea na Msami. SWAGGAZ: Ok! Vipi kuhusu uhusiano wako na mzazi mwenzako P Funk kwa sasa? KAJALA: Kawaida tu! Yeye ana maisha yake na mimi nina yangu, ameoa na mimi niko kivyangu. SWAGGAZ: Umezungumzia upande wako, vipi kuhusu mwanenu Paula, anawasiliana na baba’ake? KAJALA: Hapana na hiyo ni kwa sababu mtoto niko naye mimi. SWAGGAZ: Kwahiyo tangu uachane na P Funk, mtoto hajawahi kwenda kumuona baba yake? KAJALA: Aliwahi kwenda kipindi fulani na aliishi naye wakati huo, lakini nilipomchukua na kuishi naye hawajawahi kuonana naye tena. SWAGGAZ: Labda P Funk amewahi kutaka kuonana na mwanaye? KAJALA: Hapana… nadhani ni kwa kuwa ana watoto wengine anaona wanamtosha huyu hana haja naye. Lakini nisingependa kuendelea kuongelea hayo mambo tena. SWAGGAZ: Vipi uhusiano wako na mumeo Faraji aliyeko gerezani? Je, huwa unakwenda kumtembelea? KAJALA: Nilikuwa nakwenda kumwangalia lakini kwa sasa nisiwe muongo, nina muda kidogo kutokana na kazi za hapa na pale, nimejikuta sijaenda kumuona lakini mwanzo nilikuwa nakwenda kila Jumamosi na Jumapili. SWAGGAZ: Mara ya mwisho kwenda ilikuwa lini? KAJALA: Mwezi mmoja umepita sasa. SWAGGAZ: Vipi mipango yako ya kiuhusiano? Maana mumeo yupo jela. Utamsubiri atoke muendelee na uhusiano wenu au unatarajia kuingia kwenye ndoa mpya? Nimekuuliza hili kwa sababu hivi karibuni ulisema unatamani kupata mtoto wa kiume. KAJALA: Hiyo siwezi kuongelea in public (hadharani) kwa sababu ni maisha yangu binafsi. SWAGGAZ: Ahsante sana kwa ushirikiano wako. KAJALA: Nawe pia karibu tena.
1
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM WAZAZI ambao watoto wao watapotea katika kipindi cha sikukuu watalisaidia Jeshi la Polisi, ikiwamo kutoa maelezo ni kwa nini wamepotea. Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi, Advera Bulimba, alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari. “Tutawaita watusaidie wakati watoto wanapotea wao walikuwa katika mazingira gani, maana imekuwa ni kawaida kipindi cha sikukuu vituo vya polisi vinajaa watoto waliookotwa katika maeneo mbalimbali, ikiwamo fukwe za bahari,” alisema. Aidha, aliwataka wananchi kuepuka kulewa kupita kiasi, hasa wale wanaoendesha vyombo vya moto na kwamba wakikamatwa sheria itachukua mkondo wake. “Kwa ujumla wananchi wajue kwamba jeshi lao limejipanga kikamilifu kuimarisha ulinzi nchini kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama kuelekea msimu huu wa sikukuu. “Uzoefu unaonyesha sikukuu za mwisho wa mwaka huambatana na vitendo vinavyohatarisha usalama wa raia na mali zao, utumiaji wa vilevi kupita kiasi, utapeli, wizi, unyang’anyi na uendeshaji wa vyombo vya moto bila kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani, askari watafanya doria wakati wote,” alisema. Aliwataka pia watu wanaomiliki nyumba za kulala wageni na maduka makubwa kama vile hoteli na ‘supermarket’ kufunga kamera za usalama. “Wafunge kamera ili waweze kufuatilia kila kinachoendelea katika maeneo yao, nani kaingia, nani katoka na anafanya nini,” alisema. Pia, aliwaonya wafanyabiashara wanaomiliki kumbi za starehe, huku likiwataka kuzingatia masharti ya leseni zao walizopewa hasa msimu huu wa sikukuu. Amewataka wamiliki wa kumbi za starehe wazingatie kiwango cha idadi ya watu wanaoruhusiwa kuingia ukumbini na iwapo watagundulika kuzidisha watachukuliwa hatua kali za kisheria. “Tumegundua katika msimu wa sikukuu kuna baadhi ya watu hupenda kuitumia fursa hiyo kujipatia kipato kisicho halali. “Tutapita hadi kwenye kumbi za starehe, tukikuta mtu ameruhusu watu zaidi ya kiwango cha leseni yake tutamchukulia hatua za kisheria,” alisema.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa yote inayolima korosho nchini, wahakikishe wanasimamia vizuri zao hilo na wasiruhusu kuingizwa kwa mfumo mpya wa ununuzi ambao haujaeleweka kwa wadau na wanunuzi.“Mabadiliko ya mifumo yalitolewa na baadhi ya viongozi ambao sio waaminifu, serikali iko macho itawachukulia hatua viongozi wa vyama vya ushirika wasiokuwa waaminifu. Tunataka mfumo wenye manufaa ndio utumike,” amesema Majaliwa.Alisema hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Mtwara, baada ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini, inayojengwa katika eneo la Mitengo wilayani Mtwara.Waziri Mkuu alisema msimu wa korosho kwa mwaka huu, unatarajiwa kutangazwa hivi karibuni, hivyo ni lazima kwa wakuu wa mikoa inayolima korosho, wakajiandaa vizuri ili kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima.Alisisitiza wafanyabiashara kutojihusisha na ununuzi wa korosho kwa njia ya kangomba.“Kangomba imepigwa marufuku, watakaojihusisha moto utawawakia huko huko. Tunataka wakulima wenyewe ndio wanufaike,” amesema.Pia, ametoa mwito kwa wakulima wa zao la korosho, kuendelea kujiimarisha na wahakikishe wanajiwekea akiba kwa ajili ya ununuzi wa pembejeo kwa sababu. “Serikali itaendelea kusimamia zao hili ili wakulima wapate tija,” alisema.Mapema, Waziri Mkuu ametembelea ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini na kukagua kazi ujenzi inayoendelea, ambayo alisema itakapomalizika itawapunguzia wananchi safari ya kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam kufuata huduma.Alisema serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli imejikita katika kuboresha huduma mbalimbali za wananchi zikiwemo za afya, hivyo wananchi wa Kanda ya Kusini watapata matibabu ya kibingwa karibu na maeneo yao.
3
KAMPUNI ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena East Africa Ltd imepongeza makubaliano kati ya Kampuni ya Mbolea ya YARA Tanzania, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Taasisi ya Utafi ti wa Kilimo Uyole kufanya utafi ti ya afya ya udongo kuongeza uzalishaji na mageuzi ya kilimo.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Petrobena, Peter Kumalilwa alisema kampuni yake imejipanga kushiriki kikamilifu katika kuchagiza mageuzi kwenye sekta ya kilimo kwa kumfikishia mkulima pembejeo kabla ya msimu wa kilimo kuanza. “Makubaliano hayo yataleta maana zaidi kama elimu itamfikia mkulima juu ya umuhimu wa kupima afya ya udongo kabla ya msimu wa kilimo kutambua zao gani linafaa katika eneo lake na mbolea aina gani na kiasi gani atumie shambani kwake,” alisema Kumalilwa. Kampuni hiyo ni msambazaji mkuu wa Yara.Alisema kwa kufanya hivyo mkulima atakuwa amewezeshwa kufikia malengo yake kwa kuongezeka kwa tija katika uzalishaji kutokana na kufuata kanuni za kisasa za kilimo ikiwemo kupima afya ya udongo. “Zoezi hili litarahisisha kazi kwa upande wa usambazaji mbolea kwa wakulima kwani watakuwa wanajua ni aina gani ya mbolea zinahitajika na wakulima na hivyo kuchochea uzalishaji,” alisema. Pia alisema kampuni yake imeaanza kutoa elimu kwa wakulima Morogoro juu ya matumizi bora ya pembejeo hivyo makubaliano yaliyofanyika yameiongezea nguvu kutoa mchango stahiki katika kilimo.“Malengo yetu ni kuanzisha kituo mahili kitakachotoa elimu na mafunzo juu ya kilimo cha kisasa na uhifadhi wa mbolea kuondoa tatizo la kukosekana mbolea katika msimu wa kilimo,” alisema Kumalilwa. Alisema wamesambaza mbolea Tabora na Morogoro kwa wakati na kumaliza malalamiko ya wakulima juu ya mbolea na kazi hiyo itakuwa endelevu kumwondolea mkulima vikwazo kufikia malengo yake.Aidha, Kumalilwa aliishukuru Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais John Magufuli kwa kushirikiana na sekta binafsi katika kuhakikisha mkulima nchini anafanya kilimo cha kisasa chenye tija. Ofisa Mazingira na Kilimo Endelevu kutoka Kituo cha Kuendeleza Kilimo Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), John Banga alisema makubaliano hayo ni utekelezaji wa Mpango wa Awamu ya Pili wa Maendeleo ya Kilimo Tanzania (ASDP -II) hali itakayochagiza maendeleo na ukuaji wa kilimo.“Makubaliano haya yanaonyesha serikali inavyoshirikiana na sekta binafsi katika kutengeneza mazingira wezeshi ili kuleta mapinduzi katika kilimo nchini na kufanikisha azma ya ujenzi wa viwanda,” alisema. Alisema SAGCOT itashirikiana na wadau wote sekta ya kilimo na mifugo kumwinua mkulima kutokana kufanya kilimo cha mazoea na kufanya kilimo cha biashara na kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi.
3
NA WAANDISHI WETU TIMU za Yanga, Simba na Azam zimeendeleza wimbi la ushindi na kukabana koo kileleni mwa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya jana kushinda mechi zao za pili mfululizo. Timu hizo zote zina pointi sita, lakini zinatofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa. Yanga ambao wanatetea ubingwa hadi sasa ipo kileleni ikiwa haijaruhusu bao la kufungwa, ila imeshinda mabao matano hadi sasa, ikifuatiwa na Azam ambayo imeshashinda mabao manne na kuruhusu moja la kufungwa. Simba inafuata katika nafasi ya tatu, ikiwa imeshinda mabao matatu na kutoruhusu bao, wakati Mtibwa Sugar na Majimaji nazo zina pointi sita katika nafasi ya nne na tano. Yanga iliyokuwa nyumbani kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, iliifunga Tanzania Prisons mabao 3-0, Simba yenyewe ikalipa kisasi kwa kuichapa ugenini Mgambo JKT mabao 2-0. Azam nayo iliyokuwa ugenini kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga ilizidi kumweka pabaya kocha wa Stand United, Mfaransa, Patrick Liewig baada ya kuwachapa mabao 2-0. Mkenya Allan Wanga alifungua akaunti ya mabao Azam kwa kuifungia bao la kwanza, kabla ya kiungo, Frank Domayo kufunga la pili kuelekea mwishoni mwa mchezo huo. Yanga ilianza kwa kasi mchezo huo dhidi ya Prisons ikitaka kupata bao la mapema, lakini kadiri muda ulivyokuwa unakwenda walipungua makali na kuiga mpira wa polepole waliokuwa wakicheza Tanzania Prisons. Hadi dakika 25 za kwanza zinamalizika timu zote zilionekana kucheza sana katikati ya uwanja na kufanya mashambulizi yasiyokuwa na maana hali iliyopelekea kutopigwa shuti lolote lililolenga lango wala kutoka nje. Yanga ilicharuka na kufanya shambulizi kali dakika ya 26 langoni mwa Prisons, ambapo mpira uliomponyoka kipa wa maafande hao, Mohamed Yusuf, ulimkuta beki Mbuyu Twite aliyepiga shuti kali lililotinga wavuni. Kipa wa Prisons, Yusuf alifanya makosa mengine dakika ya 44 baada ya kuokoa vibaya mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na kiungo, Thabani Kamusoko, uliomkuta Amissi Tambwe na kufunga bao la pili kwa kichwa na mpira kwenda mapumziko kwa Yanga kuwa kifua mbele kwa mabao hayo. Kocha wa Prisons, Salum Mayanga, alifanya mabadiliko kipindi cha pili kwa kumtoa kipa wake aliyepwaya, Yusuf na kuingia Aron Kalambo, kisha akamtoa tena Mohamed Mkopi na kuingia Cosmas Ader. Mwamuzi wa mchezo huo, Alex Mahagi wa Mwanza, alimuonyesha kadi ya njano Lambert Sibianka wa Prisons kwa kumfanyia madhambi, Deus Kaseke, dakika ya 59 alimpa tena kadi ya njano James Josephat kwa kumkwatua Kamusoko. Yanga iliyoonekana kuimarika kipindi cha pili, ilipata penalti dakika ya 60 kufuatia James kumkwatua Simon Msuva aliyekuwa anaelekea kufunga, iliyopelekea mwamuzi kumuonyesha beki huyo kadi nyekundu iliyotokana na kadi ya pili ya njano, penalti hiyo ilifungwa vema na Donald Ngoma dakika ya 62 likiwa ni bao lake la pili msimu huu. Kwa upande wao Wekundu wa Msimbazi Simba, iliyoendeleza kuzitesa timu za Tanga kwenye Uwanja wa Mkwakwani msimu huu ikianza kwa kuichapa African Sports bao 1-0 wikiendi iliyopita, kabla ya kuilaza Mgambo JKT na kulipa kisasi cha kufungwa nayo mabao 2-0 msimu uliopita kwenye uwanja huo. Mabao ya Simba kwenye mchezo huo yalifungwa na Mzimbabwe, Justice Madjavi dakika ya 27, aliyeunganisha krosi ya beki Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ kwa kichwa, kabla ya Mganda Hamis Kiiza kufunga bao lake la pili msimu huu dakika ya 73 kwa shuti kali la kiufundi lililomshinda kipa wa Mgambo, Said Abdi. Kocha wa Simba, Dylan Kerr, alimuingiza kipindi cha pili mshambuliaji wake Msenagal, Pape N’daw kwa kumpa dakika tatu za mwisho za mchezo huo, lakini hakuonyesha lolote la maana hadi mpira huo ulipomalizika. Matokeo mengine, Ndanda iliutumia vema uwanja wake wa Nangwanda Sijaona kwa kuichapa Coastal Union ya Tanga bao 1-0 lililofungwa na mshambuliaji, Atupele Green, Mtibwa Sugar ikaendeleza wimbi la ushindi kwa kuichapa Toto African mabao 2-1 ugenini katika Uwanja wa Kirumba, Mwanza. Mkoani Mbeya kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya City ilirekebisha makosa yake ya kufungwa mchezo wa kwanza kwa kuifunga JKT Ruvu mabao 3-0, yaliyofungwa na Joseph Mahundi, Themi Felix na David Kabole. Mwadui iliyoanza kwa kuchapwa ugenini, ilirejea kwenye dimba lake la Mwadui Shinyanga na kuipa kichapo cha pili msimu huu African Sports cha mabao 2-0, huku Majimaji iliendeleza wimbi la ushindi kwa ushindi nyumbani kwa kuichapa Kagera Sugar bao 1-0.   Vikosi Yanga: Ally Mustafa, Mbuyu Twite, Haji Mwinyi, Nadir Haroub, Kelvin Yondani, Thabani Kamusoko, Simon Msuva, Haruna Niyonzima/Geofrey Mwashiuya (dk 80), Amissi Tambwe/Malimi Busungu (dk84), Donald Ngoma na Deus Kaseke/Salum Telela (dk 66) Prisons: Mohamed Yusuf/Kalambo (dk 46), Salum Kimenya, Laurian Mpalile, James Josephat (kadi nyekundu dk 61), Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil, Lambert Sabianka, Juma Seif, Mohamed Mkopi/Ader (dk 47), Boniface Hau na Jeremia Juma.  
4
NIMESHAKUTANA na wazazi wengi wanaolalamikia tabia ya ukorofi wa watoto wao. Hawa ni watoto wepesi kurusha rusha mikono na miguu kama namna ya kupinga unachowaelekeza kufanya. Huwa wana ushindani, wagomvi wanapokuwa na wenzao. Ukorofi unakwenda sambamba na tabia ya kupenda kujiona ni mtawala anapokuwa na wenzake. Matokeo yake ni migogoro na wenzake mara kwa mara. Ukorofi, kwa hakika, ni ujumbe. Ukorofi ni lugha ya kusema moyo wa mtoto unakosa kitu fulani anachokihitaji. Ni sawa na mtu aliyeshinda njaa siku kadhaa. Kwa vyovyote vile ni dhahiri atakosa utulivu. Mwili wake utahitaji chakula. Mtoto mkorofi kimsingi anaamini watu wanaomzunguka hawajatambua nafasi yake ipasavyo. Ndani yake mna sauti inayomwaminisha kuwa hatambuliki. Imani hiyo potofu huchochea jitihada za kutafuta kutambulika kwa namna isiyokubalika. Ubishi na ukaidi anaoufanya wakati mwingine bila hata yeye kujua anafanya nini ni namna ya kujirudishia mamlaka anayoamini hana. Anapobishana na mzazi, anapogombana na wenzake, kimsingi anajaribu kujirejeshea ushawishi ambao anaamini hana. Mambo mengi yanaweza kuzaa ukorofi. Wapo baadhi ya wanataaluma wanaamini mtu huzaliwa na ukorofi. Inawezekana. Lakini kwa sehemu kubwa tafiti zinaonyesha kuwa ukorofi ni zao la malezi. Hapa kuna mambo makubwa matatu. Kwanza, inawezekana kwa sababu ya ku tamani mtoto ‘anyooke’ umekuwa na sheria kali mno. Unaamini mtoto hawezi kufanya kitu bila kuamrishwa. Kwa sababu ya kuamini hivyo, umejikuta ukijenga mazingira ya mapambano yasiyo na sababu. Lakini pili, inawezekana ikawa ni mazingira ya malezi. Hapa tunazungumzia wazazi au watu wanaoishi na mtoto kuwa na tabia za ukali, ugomvi, kutokujali, na aina nyingine za matumizi ya mabavu. Kwa kawaida, watoto wananasa kwa haraka sana mambo yanayogusa hisia zao. Wanapoona mtu mzima anafanya jambo fulani na watu anaowaamini wanalichukulia kawaida, wanakuwa na uwezekano mkubwa wa kufanya kile kile wakati fulani. Bila kujali chanzo chake kuna hatua za kuchukua kushughulikia ukorofi. Kwanza wekeza katika kujenga urafiki. Hatuzungumzii urafiki wa siku mbili au tatu. Tunazungumzia urafiki wa kudumu ambao mtoto hatakuwa na sababu ya kuwa na mashaka nao. Kama tulivyoona, mtoto mtundu kimsingi analo hitaji kubwa la uhusiano wa karibu na wewe mzazi. Unapojitahidi kuwa karibu naye usishangae mwanzoni bado mtoto akaendelea kuwa mkaidi vilevile. Usikate tamaa. Mpe nafasi ya kukuamini kwa kujenga urafiki imara. Sambamba na urafiki, punguza amri na kelele zisizo za lazima. Kumbuka kuwa amri bila urafiki huchochea uasi. Badala yake jenga tabia ya mazungumzo ya utulivu unaposhughulika naye. Badala ya kuagiza, jaribu kushirikiana naye. Mwonyeshe kuwa unajali na kuthamini kile anachokipenda. Kumbuka ukorofi wake unato- kana na hali ya kujisikia kutokue- leweka. Kwahiyo katika mazungumzo mpe nafasi ya kusema. Mwache aongee yaliyoujaza moyo wake na usiwe mwepesi kukosoa hisia zake wala kujitetea. Mpe uzingativu kwa kuacha shughuli unazofanya kwa ajili yake. Ushirikiano wa kiwango hiki utamchangamsha. Ukiweza kufanya hivi bila unafiki mtoto ataanza kukuamini na kidogo kidogo atabadilika. Pia mheshimu kama mtu mwingine yeyote unayemheshimu. Heshima ina mambo mengi. Usimdhalilishe mbele ya wenzake kwa maneno au vitendo. Kama kuna sababu ya kumwadhibu, fanya hivyo kwa staha. Kumheshimu mtoto hakukuondolei mamlaka yako kama mzazi. Aidha tengeneza mazingira ya kumshirikisha kwenye maamuzi. Kwa sababu tayari ana utundu, mweke karibu unapotaka atekeleze jambo. Badala ya kumwambia ‘kafanye,’ badili lugha iwe, ‘tufanye’ hata kama hulazimiki kufanya. Inapobidi hasa kwenye hatua za mwanzo, shirikiana naye kufanya hicho unachotaka akifanye. Christian Bwaya ni mhadhiri wa Saikolojia Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWE- CAU). Twitter: @bwaya, Simu: 0754870815
0
['Paris St-Germain imesema kuwa itachukua hatua kali baada ya mshambuliaji wa Brazil Neymar kufeli kuhudhuria mazoezi ya kwanza ya timu hiyo.', 'Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alitarajiwa kurudi katika mazoezi siku ya Jumatatu.', 'Mshambuliaji huyo amehusishwa na uhamisho kurudi klabu yake ya zamani ya Barcelona.', '"Paris St-Germain imesema kuwa Neymar Jr hakuhudhuria kikao cha kwanza cha mazoezi kulingana na muda na eneo la mazoezi hayo. ', "''Hii ni kinyume na matarajio ya klabu hiyo'' , ilisema taarifa. ", "''Klabu hii inajutia hatua hiyo''.", 'Neymar alijiunga na PSG kutoka Barcelona kwa dau lililovunja rekodi la £200m mnamo mwezi Agosti 2017. ', 'Ameifungia klabu hiyo magoli 34 katika mechi 37 na kuisaidia kushinda mataji ya ligi ya kwanza lakini pia amehusishwa na makosa kadhaa ya utovu wa nidhamu ikiwemo kupigwa marufuku kwa mechi tatu kwa kumkemea shabiki baada ya PSG kushindwa katika kombe la ligi ya Ufaransa.', 'Pia atakosa kushiriki mechi tatu za Ulaya kwa kumtusi afisa wa mechi.', 'Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Santos nchini Brazil alivuliwa unahodha mnamo mwezi Mei kabla ya kupata jeraha la kifundo cha mguu wakati wa mechi ya kirafiki dhidi ya Qatar ambayo ilimfanya kukosa michuano ya Copa America ambayo taifa lake ndilo lililoibuka mshindi nyumbani.', 'Wiki iliopita rais wa Barcelona Josep Bartomeu alidai kwamba Neymar anataka kuondoka PSG msimu huu.', 'Kulingana na ripoti katika vyombo vya habari vya Uhispania , Neymar amekubali kupunguziwa mshahara wake kwa Yuro 12m ili kusaidia katika kurudi katika klabu yake ya zamani katika uwanja wa Nou Camp ambapo alicheza kati ya mwaka 2013 hadi 2017. ', 'Mabingwa hao wa Catalan tayari wamewasajili Frenkie de Jong kutoka Ajax kwa dau la £67m msimu huu na wanadaiwa kuwa na hamu ya kumsaini mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann kutoka Atletico Madrid.']
4
KOCHA msaidizi wa timu ya Yanga Noel Mwandila baada ya kupata pointi tatu dhidi ya Coastal Union mwishoni mwa wiki iliyopita, amsema rasmi sasa wamefungua mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa mwaka 2019/20.Yanga iliibuka na ushindi huo kwenye uwanja wa Uhuru Dar es Salaam baada ya kufanya vibaya katika mechi mbili za mwanzo ambapo ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Polisi Tanzania.Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha pointi nne ikiwa nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 20. Simba ndio inaongoza msimamo wa kuwa na pointi 12.Mwandila alisema walianza ligi hiyo kwa kusuasua kwa kupoteza mchezo mmoja na mwingine kutoka sare hivyo walipoingia kwenye mchezo uliopita aliwapa maelekezo wachezaji wake kuingia na jambo moja la kusaka pointi tatu muhimu.“Tumefanikiwa kupata pointi tatu muhimu ambazo tulikuwa tumedhamiria kuzipata na sasa tunatangaza tumeanza rasmi mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania,” alisema Mwandila anayeongoza benchi la ufundi kufuatia kocha mkuu wa timu hiyo Mwinyi Zahera kuendelea kutumikia adhabu aliyopewa na Bodi ya Ligi kwa kosa la kuvaa mavazi yasiyoruhusiwa uwanjani na kuwakejeli viongozi wa TFF.Katika hatua nyingine wachezaji wa kikosi hicho walizawadiwa kitita cha Sh. Million 10 kurudisha morali ya kuendelea kupambana na kila mchezo kuhakikisha wanapata pointi tatu muhimu.Fedha hizo zilitolewa na mdhamini wa timu hiyo GSM na kukabidhiwa na mwenyekiti wa timu hiyo Mshindo Msolla aliyedai kila timu hiyo watakapo kuwa wanavuna pointi tatu basi zitakuwa zinanunuliwa kwa kitita cha sh milioni 10.
4
TIMU ya taifa ya soka ya wanawake ya Uganda, Crested Cranes, imetolewa katika mbio za kufuzu kwa michezo ya Olimpiki itakayofanyika Tokyo 2020 baada ya kufungwa jumla ya mabao 4-2 dhidi ya Ethiopia.Katika mchezo wa juzi uliofanyika jijini hapa kwenye Uwanja wa Lugogo, Uganda ilipoteza mchezo huo wa pili baada ya kufungwa bao 1-0. Bao hilo pekee katika mchezo huo lilifungwa na Loza Abera. Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Ethiopia, Uganda walifungwa 3-2 Jumatano iliyopita.“Somo tulilojifunza kutoka katika mchezo huu sio kwa ajili yetu lakini ni kwa ajili ya huko mbele, kwani huko mbele timu yetu tutaibadili,” alisema Bulega alipozungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo huo. Ethiopia sasa itakutana na Cameroon katika raundi ya pili ya kusaka timu tano zitakazofuzu kwa michezo hiyo. “Kwetu sisi huo sio mwisho.Tulicheza na wapinzani bora zaidi lakini timu yetu ina mwelekeo mzuri mbele. Na sisi tutapata nafasi ya kucheza na timu kubwa pia,” alisema Bulega. Bulega ilifanya mabadiliko matano katika timu hiyo, ambapo alianza na kumtoa nahodha Tracy Jones Akiror (mabadiliko yaliyowashangaza wengi), Resty Nanziri, na wengine watatu Hasifah Nassuna, Fauziah Najjemba na Fazilah Ikwaput na ndio iliwagharimu.
4
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imejizatiti kuimarisha ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini kwa kuwa na maabara bora zitakazochunguza bidhaa hizo kwa ajili ya kuwalinda walaji.Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda, Hassan Hafidh Khamis katika sherehe za uwekaji msingi jengo la maabara ya bidhaa mbalimbali linalomilikiwa na Shirika la Viwango la Zanzibar (ZBS).Amesema wakati Zanzibar ikielekea katika kutekeleza dhana ya uchumi wa viwanda vya kati, suala la kukuza na kuimarisha viwango limepewa kipaumbele cha kwanza.Alifahamisha kwamba baadhi ya bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali Zanzibar zinakosa kuingia katika soko la utalii kwa sababu ya kukosa viwango.Alisema yamekuwepo mafanikio makubwa katika uzalishaji wa bidhaa kwa wajasiriamali lakini tatizo kubwa ni ukosefu wa utaalamu unaohitajika katika masuala ya viwango.“Tunataka kuingia katika uchumi wa viwanda kwa kuwa na maabara zitakazokuwa na viwango vya kuzalisha bidhaa mbalimbali na kumudu ushindani wa soko,” amesema.Aliwataka wafanyabiashara nchini kushirikiana na taasisi ya viwango ili kudhibiti uingizaji wa bidhaa zilizopita wakati wake na kusababisha madhara makubwa kwa jamii.Mkurugenzi wa ZBS Khatib Mwadini alisema Zanzibar imepata mafanikio makubwa katika masuala ya viwango tangu kuanzishwa kwa shirika hilo mwaka 2011.Alisema ujenzi wa maabara za taasisi ya viwango unahusisha majengo mawili ambapo ujenzi wake utakapomalizika utakuwa na maabara tisa.Amezitaja maabara zitakazojengwa katika jengo A ni maabara ya vifaa vya ujenzi, maabara ya kupimia zege, maabara ya saruji na maabara ya kupimia nondo na ubora wake.Aidha alisema jengo B litakuwa na ofisi za maabara ya nguo na ngozi, maabara ya kemikali, maabara ya chakula pamoja na vimelea na maabara ya umeme.“Majengo hayo mawili ya ghorofa yatakuwa na maabara kwa ajili ya kupima vifaa vyenye mahitaji ya aina hiyo,” amesema.Majengo hayo mawili ya Ofisi ya Maabara ya Taasisi ya Viwango Zanzibar (TBS) ujenzi wake utagharimu jumla ya Sh bilioni 1.3.
5
KOCHA mkuu wa timu ya Soka ya taifa ya wanawake Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens ,Bakari Shime amesema morali ya kikosi hicho ipo juu tayari kwa kuwakabili Sudan Kusini kwenye mchezo wao wa kwanza wa kundi A katika michuano ya kombe la Chalenji.Michuano hiyo inayofanyika chini ya usimamizi wa Baraza la vyama vya soka Afrika Madhariki na Kati, Cecafa inatarajiwa kuanza Jumamosi ya wiki hii kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi ikishirikisha timu nane. Queens ambao ni mabingwa watetezi mara mbili mfululizo watakuwa na kibarua hicho mbele ya Sudan siku ya ufunguzi wa michuano hiyo na tayari kikosi hicho kipo kwenye maandalizi kabambe.Akizungumza jana Dar es Salaam Shime alisema morali ya kikosi ipo juu pamoja na kwamba mazoezi mepesi yanaendelea kutolewa kwa kikosi hicho.“Morali ya kikosi cha Queens ipo juu na kwa sasa kwa vile muda bado benchi la ufundi tunaendelea kuwapa mazoezi mepesi kuweka sawa miili yao tayari kwa mchezo wetu ambao tunahitaji zaidi ushindi kubusti malengo yetu,” alisema Shime .Alisema mazoezi anayoendelea kuwapa vijana hao ni namna ya kutoa pasi imfikie mlengwa kwa wakati pamoja na kuwaelekeza nidhamu kwa muda wote wakiwa uwanjani. Shime alisema pamoja na kwamba mechi hiyo itakuwa na upinzani bado anaamini ubora wa mchezaji mmoja mmoja unaweza kuwapa majibu sahihii hususan kwenye kuamua matokeo uwanjani.Timu nyingine zinazoshiriki michuano hiyo ni Tanzania Bara, Zanzibar,Burundi na Sudan zilizo kundi A na kundi B likiwa na timu za Ethiopia, Kenya, Uganda na Djibouti.
4
Mkurugenzi Mkuu wa ATCl, Ladislaus Matindi amesema wamejipanga vizuri ili kujitanua kibiashara na kurudi katika mfumo wa kimataifa wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Ndege (IATA).Amesema ATCL iliondolewa katika mfumo wa kimataifa wa utoaji wa huduma na ununuzi wa tiketi kwa kukabiliwa na madeni makubwa.Kwa mujibu wa Matindi, madeni ambayo yaliitia hasara kubwa ATCL yalitokana na udanganyifu wa mikataba ya huduma, manunuzi na ukodishwaji wa ndege.Amesema kitendo cha kutia saini na kampuni hiyo maana yake sasa ATCL itarudi tena katika utoaji wa huduma zake mbalimbali kwa kutumia mgongo wa kampuni hiyo inayoheshimika duniani.Matindi amesema, taratibu zote zimefuatwa katika makubaliano na watoaji wa huduma za ndege za kimataifa Hahn Air, ikiwemo kupata baraka ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kuridhia.Awali Makamu wa Rais wa kampuni hiyo, Steve Krackstedt amesema, wameingia mkataba na ATCL baada ya kuridhishwa na juhudi zake kujiimarisha ili kurudi mfumo wa kibiashara.Amesema kazi kubwa imefanywa na ATCL kuimarisha huduma zake ikiwemo kununua ndege mpya kwa ajili ya safari zake nchini na nje ya nchi ikionesha utayari kufanya biashara.
5
UONGOZI wa Halmashauri ya Itigi mkoani Singida umesema utawachukulia hatua kali wakusanyaji ushuru wote watakaobanika kushindwa kuwasilisha benki kwa wakati makusanyo yao yote ya mapato kama ambavyo sheria na kanuni za fedha zinawataka kufanya.Hatua hizo zimetajwa kuwa ni pamoja na kuwafukuza kazi mara moja wote watakaopatikana na makosa na hatimaye kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Itigi, Pius Luhende alitoa ahadi hiyo mbele ya wajumbe wa baraza la kawaida la madiwani lililofanyika mjini hapa kujadili utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika kipindi cha Julai hadi Desemba mwaka jana. “Naomba tuaminiane waheshimiwa madiwani. Hakuna mkusanyaji ushuru hata mmoja atakayekwepa kuchukuliwa hatua iwapo atagundulika kuwa na upotevu wa fedha yoyote aliyokusanya,” alisema.Alikuwa akijibu hoja mbalimbali za madiwani ambao walidai kuwa mapato ya halmashauri hiyo yamekuwa yakipotea. Walidai kuwa baadhi ya wakusanyaji ushuru wameshindwa kuwasilisha benki kiasi kikubwa cha fedha ikilinganishwa na idadi halisi iliyopo kwenye mashine maalumu za kukusanyia mapato kielektroniki (POS). Mkurugenzi Mtendaji huyo alieleza kuwa kutokana na baadhi ya wakusanyaji ushuru kutokuwa na elimu ya kutosha juu matumizi ya mashine hizo za kukusanyia ushuru kielektroniki, huenda idadi ya fedha inayodhaniwa kutowasilishwa benki ikawa sio sahihi.“Ninyi ndio mliowapendekeza wakusanyaji ushuru hawa kwenye maeneo yenu, leo mnataka tuwaondoe. Sawa, nakubaliana nanyi, lakini ni vizuri tukawa na wakusanya ushuru wa mikataba ili tuweze kuwabana na kuwawajibisha kisheria kulingana na mikataba yao” alishauri.Awali, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Ally Minja alifahamisha kuwa katika kipindi cha Julai hadi Desemba mwaka jana, jumla ya Sh milioni 789.96 zilikusanywa kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ya ndani, ikiwa na sawa na asilimia 41 ya lengo la kukusanya Sh bilioni 1.94. Alisema moja ya sababu kuu ya mapato ya ndani kuwa kidogo inatokana na halmashauri kuwa na vyanzo vichache vya uhakika. Alisisitiza umuhimu wa kubuni vyanzo vipya, kusimamia, kufuatilia kwa karibu fedha zinazokusanywa na kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha hizo.
3
WANAFUNZI watatu wa Chuo Kikuu Mzumbe (MU) kilichopo mkoani Morogoro wamejinyakulia kitita cha Sh 1,000,000 kila mmoja baada ya kuwashinda wenzao kwenye shindano la kushindanisha mawazo bora zaidi ya ubunifu.Shindano hilo lilifanyika hivi karibuni na kushuhudiwa na Waziri wa Elimu , Sayansi na Tenkolojia , Profesa Joyce Ndalichako wakati wa kilele cha ufungaji kambi ya vijana ya ujasiriamali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe. Mkuu wa Idara ya Rasilimali na Ulezi wa Chuo Kikuu hicho, Dk Emmanuel Chao, alisema kwa mara ya kwanza katika kambi ya mwaka huu Chuo Kikuu hicho kimetenga fedha kwa ajili ya kushindanisha mawazo bora sita ili kupata mawazo bora zaidi matatu ambayo yatapatiwa zawadi ya Sh milioni moja kila mmoja.Dk Chao alisema kwa sasa wanatoa elimu ya vitendo na kuwajengea uwezo na nyenzo ili waweze kufanya vizuri katika ujasirimali wao . Mshindi wa kwanza katika shindano hilo ni Nyanjala Maingu “asante mama batiki” aliyewasilisha wazo la ubunifu la namna ya kuzalisha batiki na kutengeneza makoti ya wanawake, mshindi wa pili alikuwa ni Anthony Michael ambaye wazo lake la ubunifu lilikuwa ni la namna ya kutengeneza mfumo wakuunganisha wahitaji wa magari ya mizigo na huduma hiyo kutumia simu ya mkononi na aliyenyakua nafasi ya tatu ni mwanafunzi mwingine wa Chuo Kikuu hicho aliyenyakuwa nafasi tatu Rabia Luhuna aliyeshinda kwa wazo lake la ubunifu juu ya kazi za mikono la kuokota chupa za plastiki na kutengeneza mapambo.Mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo kikuu hicho ,Fatuma Mbaga ambaye ni mjasirimali alisema kuwa baadhi ya wahitimu wa vyuo vikuu wanashindwa kuthubutu kujikita kwenye shughuli za ujasirimali kutokana na woga na kukosa taarifa muhimu za namna ya kuendesha shughuli zao. Hivyo aliwashauri wanafunzi wanaosoma chuoni hapo watumie vizuri simu zao ‘simu janja’ ili kupata taarifa mbalimbali zinazohusiana na masuala mbalimbali ya ujasilimali .Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Lughano Kusiluka alisema mwaka 2017 Chuo hicho kilianzisha kambi ya ujasiriamali ambayo inashirikisha wanafunzi wa Mzumbe na wahitumu wa Chuo hicho ambao ni wajasiriamali. Alisema tangu kuanzishwa kwa kambi hiyo bidhaa mbalimbali zimebuniwa na kutengenezwa na wanafunzi wabunifu na wajasirimali na kuzunduliwa ambapo mwaka huu wanafunzi 48 wa Chuo Kikuu hicho wameandikisha mawazao yao ya kibunifu ili yaweze kuboreshwa.
3
Hivi karibuni Mkwasa alimpa unahodha mchezaji wa TP Mazembe ya Congo DR, Mbwana Samatta na kusema Haroub atabaki kuwa nahodha kwenye timu inayoshiriki michuano ya ndani ya Afrika (Chan).Uamuzi huo ulimfanya Haroub kutangaza kujiuzulu kucheza timu ya taifa, akisema moja ya sababu ni kupokwa nafasi hiyo.Akizungumza na gazeti hili jana, Mkwasa alisema anamheshimu Haroub na anatambua mchango wake kwenye taifa.“Sikuwa na sababu ya kumwondoa kwenye unahodha, mimi namheshimu sana Canavaro (Haroub) na ametoa mchango mkubwa kwa taifa hili na bado namhitaji, kwa nini nimuondoe,” alisema.“Nilichokifanya ni mabadiliko kidogo tu kwenye kazi, ni kama ninyi huko kuna mhariri wa habari na mhariri wa michezo, ndivyo nilivyofanya mimi na hili lipo duniani kote, hata ukiangalia wenzetu Ivory Coast, Cameroon, Zambia, Uganda na hata Rwanda… “Sasa hivi kuna mashindano ya Chan yanaendelea lazima utakuta na hodha wa Afcon sio yule wa Chan,” alisema.Akifafanua zaidi Mkwasa alisema aliamua kumpa Samatta ili kuwa, kama motisha zaidi baada ya kupata tuzo ya mwanasoka bora anayecheza Afrika.“Na ili hata akienda huko nje thamani iongezeke kwamba hachezi tu timu ya taifa lakini pia ni nahodha,” alisema.“Halafu si kweli kwamba Canavaro alipata taarifa hizo kwenye vyombo vya habari, nakumbuka nilimpigia simu tarehe 10 hata kwenye simu yangu bado inaonesha nikamueleza kwamba nimefanya mabadiliko kidogo yeye atakuwa nahodha wa Chan na Samatta atakuwa wa Afcon, aliniitikia vizuri, lakini kumbe hakufurahi mi sikujua… na sikuona umuhimu wa kumpa barua kwa sababu ni mabadiliko yaliyofanyika ndani ya timu tu humo humo,” alisema.Kuhusu kujiuzulu kwa Haroub, Mkwasa alisema huo ni utashi wa mchezaji mwenyewe hawezi kumuamulia.“Si kwamba simhitaji, namhitaji sana kwenye timu yangu, lakini kama ameamua kujiuzulu huo ni utashi wake mwenyewe tu, mimi siwezi kumuamulia, kama ameona uamuzi wake ni sahihi napaswa kuuheshimu pia,” alisema.Haroub amekuwa nahodha wa Stars kwa takriban miaka 10 akibeba mikoba kutoka kwa Mecky Maxime na Salum Swedi.Katika taarifa yake mchezaji huyo wa Yanga alisema ameamua kujiuzulu baada ya maneno kuwa mengi hasa kutokana na kipigo cha mabao 7-0 ilichokipata Stars kutoka kwa Algeria katika mechi ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia.“Baada ya mechi ile maneno yalikuwa mengi kwamba nimezeeka, umri umekuwa mkubwa hivyo nimeona bora nipumzike, lakini pia suala la kuvuliwa unahodha bila kupewa barua pia sikulifurahia kwani nimecheza kwa miaka 10 kwenye timu hii kwa nguvu zangu zote,” alisema Haroub.
4
Kocha wa Derby Frank Lampard anajiandaa kukutana na mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich kujadiliana kuhusu uwezekano wake kuchukua nafasi ilioachwa wazi na Maurizio Sarri. (Sun) Bayern Munich haijawasiliana na winga wa Real Madrid Gareth Bale,29, anasema ajenti wa nyota huyo wa kimataifa wa Wales. (ESPN) Kocha wa Derby Frank Lampard anajiandaa kukutana na mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich kujadiliana kuhusu uwezekano wake kuchukua nafasi ilioachwa wazi na Maurizio Sarri. (Sun) Bayern Munich haijawasiliana na winga wa Real Madrid Gareth Bale,29, anasema ajenti wa nyota huyo wa kimataifa wa Wales. (ESPN) Chelsea wanataka kumpatia Lampard,40, mkataba wa miaka mitatu kuwa meneja wa Stamford Bridge. (ESPN) Chelsea wamekataa dau la pauni milioni £35 kutoka kwa Barcelona na Atletico Madrid la kumnunua mshambuliaji wa miaka 30 Mbrazil Willian. (Sky Sports) Benfica imepuuzilia mbali tetesi kuwa Atletico Madrid itaipiku Manchester City katika usajili wa mshambuliaji wa Ureno, Joao Felix, 19 kwa kima cha pauni milioni £107 na kuzitaja tetesi hizo kuwa “taarifa feki”. (AS) Manchester United inapania kumlipa Paul Pogba, 26, hadi pauni nusu milioni £500,000 kwa wiki licha ya Real Madrid na Juventus kumnyatia kiungo huyo raia wa Ufaransa. (Mail) Liverpool wamepewa ishara ya kumnunu mshambuliaji wa Ufaransa Ousmane Dembele, 22, wa Barcelona endpo wataweza kulipa pauni milioni 90. (TEAMtalk) Paris St-Germain wanataka kukamilisha mchakato wa usajili wa mshambuliaji wa Barcelona Philippe Coutinho, 27, baada ya michuano ya Copa America. (AS) Coutinho pia analengwa na Manchester United lakini huenda  kutokana na heshima alionayo kwa klabu yake ya zamani ya Liverpool. (Sky Sports)Philippe Coutinho points to his ears after scoring against Manchester United Crystal Palace wamekataa dau la pauni milioni 50 iliotolewa na Manchester United kumnunua beki wake wa kulia Aaron Wan-Bissaka, 21. (Sky Sports) United pia wamepoteza matumaini ya kumsajili mlizi wa West HamIssa Diop baada ya dau lao la pauni milioni £40m kukataliwa. Mkataba huo ulihusisha mmoja wa wachezaji wa United kujiunga na klabu huyo japo haijabainika ni mchezaji yupi. (Telefoot, via Metro)Issa DiopMlinzi wa West Ham Issa Diop West Ham wameiambia Eibar kuwa wako tayari kulipa ada ya pauni milioni £13.4 kugharamia uhamisho wa kiungo wa kati wa Uhispania Joan Jordan. (Marca) Manchester City wanatafakari uwezekano wa kumsajili upya beki wa kushoto wa PSV Eindhoven Mhispania Angelino – Mwaka mmoja baada ya kumuuza kiungo huyo wa miaka 22. (Sun) Manchester United wanakaribia kufikia mkataba mpya na kiungo wa kati wa Uhispania Juan Mata, 31. (Mirror)Juan MataMata alitua Old Trafford Manchester United ikiwa chini ya ukufunzi wa kocha wa zamani David Moyes Mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, ameambiwa na kocha wa timu ya taifa yake ya taifa Roberto Martinez kwamba “hana budi kuondoka Manchester United”. (Het Laatste Nieuws – in Dutch) Mshambuliaji wa Chelsea muingereza Martell Taylor-Crossdale,19 anafanyiwa vipimo vya matibabu kabla ya kujiunga na Hoffenheim kwa mkataba wa kudumu. (Sky Sports)
4
Klabu ya Simba imelazimishwa suluhu ya bila kufungana kwenye mchezo wa ligi kuu bara dhidi ya wagosi wa kaya klabu ya Coastal Union kwenye mchezo wa 37 wa ligi kuu bara ndnai ya  uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Mchezo huo ulioisaidia Coastal Union  kupanda mpaka nafasi ya 6 kwenye msimamo wa ligi kuu bara uliisha kwa Simba kucheza pungufu baada ya beki wao timu hiyo Pascal Wawa kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kufanyia madhambi mshambuliaji wa Coastal Union Ayoub Lyanga dakika ya 75. Simba sasa inatarajia kusafiri mpaka mkoani Kilimanajoro kukipiga dhidi ya Polisi Tanzania kwenye mchezo wa kuhitimisha ligi kuu bara msimu wa 2019/20 ambayo imekuwa ligi ya kwanza kuwa na timu 20. Baada ya mchezo dhidi ya Polisi Simba itajipanga kucheza na Namungo FC kwenye mchezo wa fainali ya kombe la shirikisho mkoani Rukwa kwenye uwanja wa Nelson Mandela  mnamo Agosti mosi.   Ubingwa tayari, tunakamilisha ratiba 😎 FULL TIME: Coastal Union 0-0 Simba SC#VPL #NguvuMoja pic.twitter.com/BKqb1oFl6L — Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) July 23, 2020
4
Katika hafla ya kukabidhi nyumba hizo jana, Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema mpango wa ujenzi wa nyumba hizo ni endelevu mpaka hapo ekari 300 zilizotengwa kwa ujenzi zitakapojengwa nyumba kwa mpango wa kuchangiana.Taalib alisema aina za nyumba zinazojengwa kwa sasa ni za matofali ya saruji ya chumba kimoja kwa Sh 750,000, nyumba za vyumba viwili na sebule kwa Sh milioni 3.8 na nyumba kubwa ya Sh milioni. 6.4.Alisema kipa wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa, Hamisi Kinye anatarajiwa kukabidhiwa nyumba yake Desemba mwaka huu pamoja na wasanii wengine Lilian Ndelwa, Edson Mwela, Happyness Magese, Asheri Kazeba, Jaqueline Joseph na Suzan Moshi ambao wamebadilisha nyumba walizokuwa wakabidhiwe za udongo na sasa watachukua nyumba zilizojengwa kwa saruji.Mwenyekiti Taalib alisema SHIWATA imeandaa mpango mkakati wa kuingiza umeme na maji katika kijiji hicho kabla ya Desemba na tayari kikundi cha wasanii kimepiga kambi ya kujiandaa kurekodi tamthiliya ya Maisha ya Bongo katika kijiji hicho.
4
UBALOZI wa China nchini umetoa msaada wa vyerehani 330 kwa vikundi vya wanawake katika mikoa sita, na vifaa 380 vya watu wenye ulemavu vyote vikiwa na thamani ya Dola za Marekani 51,617 (takribani Sh milioni 121.3).Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Balozi wa China nchini, Wang Ke alisema misaada hiyo ambayo inatolewa chini ya Programu ya RAFIKI imelenga kuwainua wanawake na kuwasaidia kukabiliana na changamoto za watu wenye ulemavu.Kwa mwaka huu kupitia programu ya Rafiki, China imetoa vyerehani 330 ambapo kati ya hivyo, 180 vinitumia umeme vikiwa na thamani ya yuan 800 kila kimoja na vyerehani 150 ni vya kawaida ambapo kila kimoja thamani yake ni yuan 700. Mikoa itakayonufaika na msaada huo ni vikundi vya wanawake kutoka mikoa ya Kilimanjaro, Dar es Salaam, Dodoma, Simiyu na Tabora.Vifaa vya watu wenye ulemavu vina thamani ya Dola za Marekani 15,000. “Kuna usemi usemao ukimuelimisha mwanaume utakuwa umemwelimisha mtu mmoja lakini ukimuinua mwanamke utakuwa umeisaidia familia nzima. Sisi tumeona tuwasaidie wanawake wa mikoa sita vyerehani, tunajua kwa kufanya hivyo wataweza kuinuka kiuchumi, kuhudumia familia zao na kulipa ada za watoto.Balozi Ke alisema katika kuendeleza ushirikiano huo, China inashirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuboresha Chuo cha Usafirishaji (NIT) ili kuwa Chuo Kikuu cha Usafirishaji na pia kuboresha Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama aliishukuru Serikali ya China na aliwataka wanufaika wa msaada huo kuutumia ipasavyo.
3
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imepanga Agosti 23, mwaka huu kuanza kusikiliza ombi lililowasilishwa na aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), la kuzuia kuapishwa kwa mbunge mteule wa jimbo hilo, Miraji Mtaturu (CCM).Lissu amefungua ombi hiloo dhidi ya Spika wa Bunge na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Agosti 23, mwaka huu na linasikilizwa mbele ya Jaji Sirilius Matupa.Jana Jaji Matupa alisema ombi la kuzuia kuapishwa kwa Mtaturu lipo ndani ya maombi ya msingi na lina hoja nyingi za kikatiba na kisheria. Hata hivyo, alisema hajaambiwa kwamba ndani ya siku 14 zijazo kutakuwa na mkutano wa Bunge utakaohusika na uapishwaji wa mbunge huyo mteule.Awali, Wakili wa Lissu, Peter Kibatala, aliomba mwongozo wa Mahakama hiyo kama itaweza kusikiliza maombi hayo na kutoa amri ya muda ya kuzuia uapishwaji wa Mtaturu.Alidai lengo la ombi hilo ni kulinda maombi ya msingi ambayo wajibu maombi watatakiwa kuyajibu. Akijibu hoja hiyo, Wakili wa Serikali Mkuu, Vicent Tangoh, aliomba ombi hilo lisubiri kwanza kwani ni la msingi la maombi yote. Hata hivyo, Tangoh aliomba Mahakama wapewe muda wa kujibu kiapo kinzani ili wapate busara za Mwanasheria Mkuu wa Serikali.Alieleza kuwa maombi hayo yanagusa muhimili mwingine wa serikali na Bunge hivyo wanaomba muda wa kushauriana ili waandae hati ya kiapo kinzani. Kwa mujibu wa maombi hayo namba 18/2019, Lissu anaiomba Mahakama hiyo impe kibali cha kufungua kesi ili itoe amri ya kumtaka Spika wa Bunge ampe (Lissu) taarifa yake ya kumvua ubunge.Pia anaiomba Mahakama hiyo impe kibali cha kufungua kesi ili iite taarifa ya uamuzi wa Spika wa kumvua ubunge na kisha itengue na kutupilia mbali uamuzi huo kumvua ubunge.Katika hati ya dharura, Lissu anaiomba mahakama hiyo isikilize na kutoa uamuzi wa maombi yake haraka kwani vinginevyo Mtaturu ambaye Julai 19, mwaka huu alitangazwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo kuwa mshindi, ataapishwa kushika wadhifa huo hivyo atakuwa ameathirika kwa kuwa atapoteza haki zake zote, kinga na maslahi yake yote yanayoambatana na wadhifa wake wa ubunge.Uamuzi wa kumvua ubunge Lissu ulitangazwa na Spika Ndugai Juni 28, mwaka huu, wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge, huku akitaja sababu mbili.Alizitaja sababu hizo kuwa ni Lissu kushindwa kuhudhuria vikao vvya Bunge kwa muda mrefu bila kumjulisha Spika kwa maandishi mahali aliko na ya pili Ni kutotoa taarifa za mali na madeni kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
3
NAIROBI, KENYA KATIBU binafsi wa Rais wa zamani wa Kenya, Mwai Kibaki amekanusha taarifa kwamba kiongozi huyo amelazwa katika Hospitali ya Nairobi. Katibu huyo, Ngari Gituku amesema kuwa Kibaki mwenye miaka 88 alifika katika hospitali ya Nairobi Jumatatu kwa ajili ya utaratibu wa kawaida wa  kuangalia afya yake.  “Ilikuwa ni safari ya kawaida na hakuna kitu kipya,” aliliambia gazeti la Daily Nation la nchini Kenya kwa njia ya simu. Wakati ikielezwa kuwa Kibaki anasumbuliwa na tatizo la goti baada ya kupata ajali ya barabarani huko Machakos  mwaka 2002,  Gituku kwa upande wake hakuthibitisha kama ni sababu ya sasa ya yeye kwenda hospitalini. “Kwa umri wake, wanaweza kumchunguza kitu chochote, kama macho, kibofu cha mkojo na vitu vingine,”  alisema. Chanzo kimoja cha habari ambacho kimekataa kutajwa jina kwa sababu yeye si msemaji wa familia kilisema kuwa rais huyo mstaafu hali yake inaendelea kuimarika na kwamba alikuwa katika hali ya tahadhari. Hatua ya Kibaki kufika katika hospitali ya Nairobi kulikuja katika siku ambayo Rais wa Mstaafu wa Kenya na ambaye ametawala nchi hiyo kwa muda mrefu, Daniel Arap Moi naye akirejea hospitalini hapo kutokana na kile ambacho msemaji wake Lee Njiru kusema kuwa ni “uangalizi wa kawaida”. Ingawa chanzo cha habari kutoka katika familia ya Moi kilisema kuwa kiongozi huyo ambaye ana miaka 95 alikimbizwa hospitalini hapo Oktoba 18 mwaka huu baada ya kupata tatizo la kupumua. Kwa upande wake Kibaki, ambaye ni kiongozi wa zamani wa chama cha Narc, anajiandaa kusheherekea miaka 89 ya kuzaliwa Novemba 15 mwaka huu. Mara ya kwanza alifikishwa hospitali ya Nairobi Januari 20, 2004. Timu ya wataalamu waliokuwa wakimtibu walisema kuwa walibaini kuganda kwa damu katika mguu wake wa kulia. Mwezi Agosti 2016,  kiongozi huyo wa zamani alifanyiwa upasuaji katika Hospitali ya  Netcare Sunninghill iliyoko nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kuondoa kuganda huko kwa damu katika mshipa wa kwenye shingo yake.
2
ZAIDI ya mabasi 2,840 yanayokwenda mikoa mbalimbali nchini yamefungwa mfumo maalumu wa ufuatiliaji wa mwenendo wake (VTS) na umeanza kutumika rasmi jana.Mfumo huo ulioanza Januari mwaka juzi kwa majaribio kwa baadhi ya njia, ni maalumu kubaini madereva wanaoendesha zaidi ya kasi ya mwendo wa 80 kwa saa ili kuepusha ajali zinazotokana na mwendokasi. Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na nchi kavu (Sumatra), Gilliard Ngewe alisema wakati majaribio yalihusisha mabasi yanayotoka Dar es Salaam kwenda mikoa ya Kanda ya Ziwa, hivi sasa mabasi 2,840 yote nchini yameunganishwa. Ngewe alisema utafiti mbalimbali uliofanyika, umebainisha upo umuhimu kutafuta njia za kudhibiti ajali hizo.Alisema miongoni mwa utafiti ni pamoja na uliofanywa na Sumatra kwa kupitia taasisi ya BICO ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unaoonesha asilimia 76.4 za ajali hizo zilitokana na makosa ya kibinadamu. Kwa mujibu wa meneja wa mradi huo, Godfrey Nsato mfumo huo wa VTS ni muhimu kudhibiti madereva nchini na kupunguza ajali za barabani.Alisema mfumo huo utatoa hadhari iwapo dereva atatanua njia kwa lengo la kuwahi na akiwa kwenye mwendo wa kasi itampigia ishara ya kumjulisha kuwa amezidisha mwendo, itaonesha pia iwapo dereva alikuwa akienda hovyo barabarani, kutoa taarifa ya ajali na itamtambua dereva wa basi. Alitaja faida nyingine za mfumo huo kuwa umesaidia kupunguza matukio ya ajali, kupunguza athari za ajali na kupunguza matumizi ya mafuta kwenye mabasi. Hata hivyo Nsato alisema baadhi ya madereva wamekuwa wakihujumu mfumo huo na kusababisha athari za ufanisi.Alisema pia kuna uhitaji wa maboresho ya elimu, udhibiti na usimamizi wa sheria kwa madereva na watumiaji wengine wa barabarani. Hii ni kutokana na utafiti huo kubaini kuwa baadhi ya madereva hawapatiwi mafunzo ya kutosha. Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Dk Isack Kamwele ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, alisema wadau wote nchini waungane kuhakikisha wanamaliza tatizo la ajali barabarani.Kamwele ameagiza kila mmiliki wa basi kuwa mwaminifu na kufunga mabasi yake mfumo huo na iwapo itabainika kuwa kuna waliokiuka, Sumatra iwachukulie hatua kali kwa mujibu wa sheria. Kamwele ameshauri pia magari yote ya serikali na daladala kufungwa VTS na kwamba serikali inaunga mkono juhudi za kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua zaidi kama sio kumalizika.
3
JUMUIYA ya Afrika Mashariki imetajwa kuwa ni jumuiya inayoongoza kwa ubora barani Afrika, ikilinganishwa na jumuiya nyingine ndani ya bara hilo. Jumuiya nyingine Afrika ni pamoja na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Afrika ya Kati (COMESA) na Afrika Magharibi (ECOWAS).Baada ya Jumuiya ya Ulaya (EU), Afrika Mashariki yenye jumla ya wakazi zaidi ya milioni 170 ndiyo jumuiya inayofuata kwa ubora duniani. Hii ina maana kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni ya pili kwa ubora duniani. Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Tanzania anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Damas Ndumbaro alipozungumza na gazeti hili hivi karibuni akielezea mwelekeo wa EAC.Kutokana na kuimarika kwa jumuiya hiyo, imefanikiwa kuongeza idadi ya wanachama kutoka wanachama watatu wa awali hadi kufikia wanachama sita. “Mwelekeo wa jumuiya kusema kweli unaimarika, niwaambie Watanzania na wanajumuiya ya Afrika Mashariki kuwa ukiondoa Jumuiya ya Ulaya (EU), hii ndiyo jumuiya inayofuata kwa ubora zaidi duniani, ni ya pili duniani na ya kwanza barani Afrika,” alisema Dk Ndumbaro.Alisema kukua huko ni kielelezo kuwa jumuiya inafanya vizuri na kuweza kuvutia nchi nyingine barani Afrika. Alisema pamoja na ongezeko hilo, bado kuna maombi ya nchi zaidi zinazotaka kujiunga na jumuiya hiyo kutokana na faida na fursa mbalimbali ambazo wamezibaini.Kwa mujibu wa Dk Ndumbaro kama jumuiya ingekuwa haifanyi vizuri nchi wanachama zisingeongezeka na pia nchi hizo zisingeomba kujiunga na jumuiya hiyo. Kwa upande wa michango ya nchi wanachama kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Ndumbaro alisema Tanzania imetoa mchango wake kwa asilimia 89 katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 ambao unaofikia ukingoni Juni 30, mwaka huu na kuongeza kuwa, ni matarajio kuwa asilimia 11 iliyobakia itamalizika kabla ya mwaka huu wa fedha kumalizika. Wakati huo huo, juhudi za Afrika Mashariki katika kuhudumia wakimbizi zimetambuliwa na Bunge la Afrika (PAP).Bunge hilo limetunuku nchi za Rwanda na Uganda kutokana na majukumu yao katika kuwasaidia wakimbizi na kuwatendea ubinadamu. Katika maazimio yake yaliyofikiwa kutoka katika vikao vyake, Bunge la Afrika lilitunuku Uganda nishani ya heshima kutokana na kuwahudumia wakimbizi zaidi ya milioni 1.2 kutoka katika mataifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Sudan Kusini. Kwa upande wake Rwanda ilipata heshima hiyo kutokana na uadilifu mkubwa na utu ambao wamekuwa wakiwaonesha wakimbizi katika maeneo yote ambayo nchi hizo zinahudumu. Nchi hiyo ilitajwa kama taifa la mfano katika kuwahudumia wakimbizi katika maeneo mbalimbali.
3
WATU wawili, mmoja mkazi wa Ifakara, Morogoro na mwingine Buza, Dar es Salaam wamekamatwa wilayani Temeke kwa tuhuma za kukutwa na gunia la bangi.Polisi katika Mkoa wa Temeke walilazimika kupiga risasi juu kuwadhibiti watuhumiwa hao, ambao baada ya kubaini wamekamatwa, walitaka kutoroka. Kamanda wa Polisi wa Temeke, Amon Kakwale alithibitisha tukio hilo na kueleza kuwa walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuhusu bangi hiyo na kufuatilia mwenendo wa mtuhumiwa, aliyekuwa akisafiri kwa basi kuja jijini Dar es Salaam juzi.Kakwale alisema watuhumiwa hao, Rashid Gabriel (40) mkazi wa Ifakara na Hamad Mbwana (44) mkazi wa Buza, Dar es Salaam, baada ya kukamatwa walifikishwa katika Kituo cha Polisi Chang’ombe, kuandika maelezo na uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani.Habarileo lilishuhudia tukio hilo katika eneo la Vetenari, Temeke saa moja usiku ambapo mlio wa risasi ulisikika na kusababisha taharuki ya watu kukimbia huku na kule.Baadae watu wawili wakiwa na mizigo mikubwa mitatu, walionekana wanahojiwa na polisi wakiwa chini ya ulinzi.
3
MKAZI wa Mhunze wilayani Kishapu Mkoa wa Shinyanga, Raphael Martine (34), anashikiliwa na Polisi akituhumiwa kumuua Shija Mahoiga (45), kwa  kumpiga kwa chuma kichwani, mikononi, na sehemu za mbavu.Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Richard Abwao amethibitisha mauaji hayo ya juzi saa tisa usiku, akisema mtuhumiwa alidai kwenda kwenye nyumba ya Mahoiga na kumfumania akiwa amelala na mkewe Maria Kija.Kamanda Abwao amesema wanamshikilia Martine kwa tuhuma ya kumuua Mahoiga kwa kutumia kipande cha chuma kumpiga nacho kichwani, mikononi na sehemu za mbavu upande wa kushoto.“Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi baada ya mtuhumiwa kumfumania Shija Mahoiga akiwa amelala na mkewe Maria Kija ambaye amejeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Jakaya Kikwete, Kishapu. Mbinu iliyotumika ni kuvunja mlango na kuanza kumshambulia kwa kipande cha chuma,” amesema Kamanda Abwao.Katika tukio lingine, Kamanda Abwao alisema Zainabu Shija (28) ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha Mhida, Kijiji cha Busangi katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama, ameuawa huku chanzo chake ni wivu wa mapenzi.Amesema Zainabu aliuawa hivi karibuni na mtu aliyefahamika kwa jina moja la Emmanuel akishirikiana na wenzake wawili kwa kumkata mapanga na kitu chenye ncha kali usoni na kichwani.“Chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi baada ya marehemu kukataa kurudi kwa mtuhumiwa ambaye alimfukuza kutokana na kutopata mtoto muda mrefu na kuolewa na mwanamume mwingine na kupata mtoto,” amesema Kamanda Abwao.Aidha, Kamanda Abwao amewataka wananchi kuacha tabia za kujichukulia sheria mkononi, bali waende kwenye vyombo vya sheria vianvyohusika kusuluhishwa.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi aunde timu ya wataalamu kufuatilia Sh milioni 700 zilizotolewa na serikali ili kukarabati Hospitali ya Wilaya ya Nachingwea ambazo hadi sasa hazijatumika.Kadhalika, Waziri Mkuu ameagiza timu hiyo ikague matumizi ya Sh milioni 400 zilizotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi Kituo cha Afya cha Kata ya Kilimarondo zimeisha na ujenzi haujakamilika.Alitoa maagizo hayo juzi wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha Kilimarondo, Nachingwea mkoani Lindi, baada ya kukagua ujenzi wa kituo hicho cha afya.“Serikali haitaki mzaha na fedha za umma, hivyo mkuu wa mkoa unda timu ya wataalamu kutoka mkoani waje Nachingwea kufuatilia ni kwa nini fedha zimetolewa tangu Julai ili kukarabati hospitali ya wilaya ziwe hazijatumika hadi leo.Pia tujue kama kweli bado zipo,” alisema Majaliwa. Alitoa agizo hilo baada ya Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Hassan Masala kumueleza kwamba hadi sasa Sh milioni 700 zilizotolewa na serikali, Julai mwaka huu kwa ajili ya ukarabati wa hospitali ya wilaya hazijatumika.Mbali na fedha hizo, pia mbunge huyo ameomba uchunguzi maalumu ufanyike kwenye mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kilimarondo baada ya fedha zilizotolewa kumalizika na mradi haujakamilika.Mradi huo wa ujenzi wa kituo cha afya ulitengewa Sh milioni 400 ambazo zimekwisha na zinahitajika Sh milioni 51 kumalizia, ambazo Waziri Mkuu ameagiza halmashauri ihakikishe fedha hizo zinatolewa ili kukamilisha mradi huo.Kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha afya kitakachokuwa kinatoa huduma mbalimbali zikiwemo za mama na mtoto na upasuaji kutawapunguzia wananchi kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 90 kutoka Kilimarondo hadi Nachingwea kufuata huduma za afya.Kuhusu upatikanaji wa nishati ya umeme, Waziri Mkuu alisema serikali imedhamiria kusambaza umeme katika maeneo yote ambayo hayajaunganishiwa nishati hiyo nchini yataunganishiwa, ikiwemo na Tarafa ya Kilimarondo.Waziri Mkuu alisema Rais John Magufuli anataka kuona kila nyumba ya Mtanzania inapata umeme tena kwa gharama nafuu, serikali imetenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika maeneo yote kwa gharama ya Sh 27,000 tu.Pia Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi hao kwamba hawatowajibika tena katika kulipia gharama za nguzo wala fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwa sababu tayari gharama hizo zimeshabebwa na serikali.
3
TANZANIA imetaka wakulima wapatiwe pembejeo kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa chakula kwa kuzalisha mazao kwa kutumia utalaamu wa kisasa pamoja na kuwapatia masoko ya uhakika ya chakula cha ziada.Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga kwenye Mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) uliofanyika Davos, Uswisi kuanzia Januari 22 hadi 25 mwaka huu.Katika mkutano huo uliobeba kaulimbiu isemayo ‘Kutengeneza Mazingira ya Utandawazi wa Dunia kwa ajili ya Mapinduzi ya Kisasa ya Nne ya Viwanda’, Dk Mahiga alimwakilisha Rais John Magufuli ambapo pamoja na mambo mengine, ulijadili kuhusu uhakika wa chakula na changamoto za uhaba wa chakula duniani.Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, ajenda kuu zilizojadiliwa kwenye mkutano huo ni pamoja na mapinduzi ya nne ya viwanda, agenda ya Afrika ya maendeleo, hali ya ulinzi na usalama Pembe ya Afrika, changamoto za biashara ya kimataifa, ushirikiano wa Bara la Ulaya na Afrika katika ajenda mpya ya maendeleo.Tanzania ilialikwa kuchangia mjadala unaohusu uhakika wa chakula na changamoto za uhaba wa chakula duniani pamoja na ajenda ya uwezeshaji wa mawasiliano ya simu za mkononi.Katika ajenda hiyo, Tanzania ilitoa wito wa umuhimu wa teknolojia katika kuboresha utaalamu katika sekta ya kilimo kwa ajili ya kuwawezesha wakulima wadogo waliopo vijijini.Taarifa hiyo ya Wizara ilisema kuwa Jukwaa hilo la kipekee liliwakutanisha viongozi wa serikali kutoka mabara yote duniani, taasisi na mashirika ya kimataifa, viongozi wa makampuni makubwa ya kibiashara kwa ajili ya kujadili maendeleo na mwelekeo wa uchumi duniani.Aidha, Dk Mahiga alikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa mashirika na makampuni yaliyopo Tanzania ambayo yanahitaji kupanua wigo kama vile Tigo na General Electric pamoja na makampuni yanayotafuta fursa za kuwekeza Tanzania.Dk Mahiga pia alikutana na Rais wa WEF, Borge Brende ambaye aliahidi kuwashawishi wawekezaji kuwekeza Tanzania na kuandaa jukwaa la wawekezaji wa kimataifa la Tanzania ili waje kuwekeza hapa nchini.Viongozi wengine waliokutana na Waziri Mahiga ni pamoja na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gesi yenye Makao makuu yake Atlanta, Georgia- Marekani, Scott Strazik, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya kupambana na magonjwa ya mlipuko, Richard Hatchett, Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kimataifa ya Millicom ambayo TIGO ni Tawi la kampuni hiyo, Rachel Samren pamoja na Mtanzania aliyetambuliwa na Jukwaa la Uchumi Duniani kwa mradi wa kutangaza utalii wa Tanzania kwa njia ya mtandao, Mohamed Al-Beity.
5
Na Mwandishi Wetu-MOROGORO KIONGOZI Mkuu wa Huduma ya Sauti ya Uponyaji Tanzania, Nabii Joshua Aram Mwantyala, amewataka Watanzania kuendelea kujinyenyekeza kwa Mungu kwa kuwa anaenda kuachilia uponyaji kwa taifa muda wowote. Wito huo aliutoa Kihonda mjini Morogoro, muda mfupi baada ya kuongoza maombi mfululizo ya kuliombea taifa ili Mungu akaliponye dhidi ya virusi vya corona na changamoto mbalimbali linalokabiliana nazo kwa sasa. Nabii Joshua alimwomba Mungu azidi kuwapa viongozi wakiongozwa na Rais Dk. John Magufuli, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais, Samia Suluhu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na viongozi wengine moyo wa ujasiri na afya njema ili wazidi kuwatumikia Watanzania kwa moyo wa upendo.  “Ukisoma Bibilia Takatifu kitabu cha pili Mambo ya Nyakati 1:14 inaeleza kwa kina kuwa ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu watajinyenyekeza, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi zao, na kuiponya nchi yao. “Katika hiki kitabu cha Mambo ya Nyakati, tumeona namna ambavyo ukuu wa Mungu una nguvu ya kubadili kilichoonekana hakiwezekani kuwezekana, kubadili mateso kuwa furaha, kuiponya nchi kutoka katika magonjwa mbalimbali kama maambukizi ya virusi vya homa kali ya mapafu ya corona (Covid-19) na mengine mengi, ninaamini uponyaji unaenda kutokea muda wowote kwa taifa letu,” alisema Nabii Joshua. Mbali na hayo, alisema kila Mtanzania katika kipindi hiki ambacho wanaendelea kumwomba Mungu, aendelee kuzingatia miongozo na kanuni zinazotolewa mara kwa mara na Serikali kuhusu namna ya kujikinga na virusi hivyo.
3
MFUPA uliowashinda vigogo wawili wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Yanga na Azam hatimaye Simba imedhihirisha ni mnyama mkali baada ya kuwapapasa Ruvu Shooting kwa mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Ruvu kama ambavyo alikuwa ikitamba na neno lake la kupapasa kwa maana ya kutoa kipigo, iliwahi kuwachapa Yanga bao 1-0 kwenye uwanja huo huo na Azam FC pia ilipigwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Mabatini huku ikitamba pia kuichapa Simba.Mabao ya wekundu hao yaliwekwa kimiani na Adam Miraji aliyefunga mawili na Tairone Santos. Ushindi huo unairudisha Simba kwenye uongozi wa ligi ikifikisha pointi 25 ikiwa mbele kwa tofauti ya pointi mbili dhidi ya Kagera Sugar iliyoongoza tangu juzi baada ya kushinda mchezo wake uliopita dhidi ya Lipuli na kufikisha pointi 23. Awali, katika mchezo huo wekundu hao walionekana kucheza kwa kushambulia ambapo dakika ya 39 Miraji aliifungia Simba bao la uongozi kwa kichwa baada ya kupata pasi nzuri ya Shomari Kapombe.Wapinzani wa Simba, Ruvu Shooting walikuwa wanacheza muda wote kwa kujilinda na kufanya mashambulizi ya kushtukiza na dakika ya 40 walipata nafasi baada ya Emmanuel Martin kubaki na kipa lakini alikosa utulivu baada ya kupiga mpira pembeni ya goli.Kipindi cha kwanza kilimalizika Simba ikiongoza kwa bao 1-0, ila ilikuwa na uwezo wa kuwa na mabao mengi baada ya kutengeneza nafasi mbili dakika ya 2 na 7 walizoshindwa kuzitumia. Kipindi cha pili Simba ilirudi kwa kasi na dakika ya 46 Tairone Santos akaifungia bao la pili timu yake kwa mguu akimalizia mpira wa kona uliopigwa na Francis Kahata.Aidha, dakika ya 74 Miraji akaifungia tena Simba bao la tatu pasi iliyotokana na Kahata. Ruvu Shooting licha ya kufanya mabadiliko ya kuwatoa Said Dilunga, Edward Christopher na Shaban Msala na kuingia Fully Maganga, Abdallah Mussa na Moses Shaban haikusaidia chochote. Pia, Simba iliwatoa Hassan Dilunga, Kahata na Meddi Kagere na kuingia Deo Kanda, Sharaf Shiboub na Ibrahim Ajibu.Michezo mingine iliyochezwa jana ni Azam FC iliyoibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbao jijini Mwanza, Singida bao 1-0 dhidi ya Mbeya City na Biashara United ikitoka suluhu dhidi ya Mtibwa Sugar.
4
JOSEPH HIZA NA MASHIRIKA  RAIS Donald Trump anayefahamika kwa ubilionea, ufahari, majivuno aliwahi kukana kutamka hilo, lakini ushahidi sasa umefichuka kuwa hali ya Ikulu ya Marekani maarufu kama White House ilistahili kile alichokana kukitamka. Mapema wiki hii utata uliibuka wakati Jarida la Golf Magazine lilimtuhumu Trump akisema: “White House ni jalala kweli kweli.’ Mara moja akifahamika jumba hilo kuwa kipenzi namba moja kwa Wamarekani, Trump anayejidai kuwa mzalendo namba moja, ndiyo maana kaja na sera ya Marekani Kwanza alikanusha kutoa matamshi hayo na suala hilo likatawala siasa. Lakini kauli hiyo aliyoikana kuitoa inafanana na kile wafanyakazi wa kampuni zilizopewa kazi za kufanya ukarabati na marekebisho katika maeneo mbalimbali ya Ikulu ya Marekani maarufu kama Whitehouse walichokiona. Ni kutokana na wingi wa panya, mende na wadudu wengine wadogo wadogo waliotawala katika majengo ya makazi hayo makongwe nchini humo. Licha ya ukongwe wake kutokana na heshima palipojijengea kwa kuishi mtu mwenye nguvu kuliko wote nchini humo na duniani kwa ujumla, haikutarajiwa kukutana na wadudu hao wanaoshamiri maeneo machafu. Hayo yamebainika kufuatia kutolewa kwa ripoti ya vitu vinavyopaswa kurekebishwa katika makazi hayo, ambayo kwa sasa yanamilikiwa na Rais Donald Trump. Ikulu ya White house, ambayo chombo cha habari cha NBC Washington kiliiona na kushirikisha ripoti nyingine ya mwaka uliopita ya wakati wa utawala wa Rais Barack Obama. Panya, mende, wadudu na vyoo vilivyovunjika au kuchakaa ni miongoni mwa vitu vingi vilivyoripotiwa zaidi kwa wafanyakazi wa kufanyia marekebisho na kuipamba Whitehouse. Panya wanadaiwa kuonekana katika majengo mbalimbali ikiwamo chumba cha kulia chakula cha maafisa wa jeshi la wanamaji kwa mujibu wa Brian Miller, Inspekta Jenerali wa kikosi cha huduma za jumla ambacho husimamia marekebisho katika makazi hayo ya rais. ”Mtu yeyote kati yetu ambaye anamiliki nyumba ya zamani anajua kwamba inahitaji kazi nyingi, lakini ni ajabu kukutwa kwa makazi haya ambayo yalipaswa kuwa safi. Mende walikuwa tatizo katika chumba cha kulia chakula huku wadudu wengine wadogo wakionekana katika nyumba anayoishi afisa mkuu wa jeshi kwa mujibu wa ripoti hiyo. Wadudu na mende pia walionekana katika chumba cha wanahabari huku panya na sisimizi wakionekana kwa wingi katika ofisi ya mnadhimu mkuu wa Whitehouse Mbali na kukabiliana na wadudu ,ripoti hiyo ya marekebisho ya Ikulu inaonyesha kazi nyingi zilizohitajika kufanyika baada ya utawala mpya kuingia mwanzoni mwa mwaka huu.
2
Na Markus Mpangala, WOTE hawajui kitu gani kitafanywa na Rais mpya wa Marekani, Donald Trump. Jumuiya ya Ulaya imehoji mwelekeo wa siasa za Trump, lakini haijapata jibu. Umoja wa Afrika bado unamsoma Trump, kwa kuwa haujamwelewa. Bara la Asia nao wanaendelea kumsoma Trump, hawajui atafanya nini. Hayo ni sehemu ya mambo yanayoendelea kote duniani kutokana na uongozi mpya wa Marekani. Kifupi viongozi wengi duniani ni kama wamekumbwa na ugonjwa. Ni homa ya dunia iliyoletwa na Trump. Ndani ya Marekani homa hiyo imefikia nyuzi joto 90. Hivi sasa kiongozi huyo anafanya mambo yake kwa matamshi mazito na msimamo mkali. Katika makala haya yapo baadhi ya mambo ambayo yanasababisha homa hiyo kupamba moto duniani. Mwanzoni mwa mwezi huu kabla ya kuapishwa, Trump aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook akisema: “Kama kuna Obamacare basi mimi ninayo Trump Don’t Care”. Ilikuwa kauli ya dhihaka lakini ndiyo uwasilishaji wake aliokuja kuutekeleza baada ya kukabidhiwa madaraka. Obamacare ni mpango wa Bima ya Afya ambao uliwasaidia takribani wananchi milioni 20 nchini humo. Hata hivyo, unalalamikiwa kuwa wa gharama kubwa kiuendeshaji. Huduma hiyo ilipitishwa na Bunge la nchi hiyo ikiwa ni moja ya sera za Rais Mstaafu Barack Obama, kuwasaidia watu masikini kupata huduma za afya. Chini ya utawala wa Obama alikutana na upinzani mkali kutoka chama cha Republican kilijaribu mara tatu kupiga kura ya kufutwa mpango huo bila mafanikio kwa kuwa hawakuwa na mbadala. Rais huyo mpya ameendelea kufanya mabadiliko ya kiuongozi baada ya kuwatangazia wananchi kwamba mabalozi wa nchi yao walioko kwenye mataifa mbalimbali na mashirika ya kimataifa wanatakiwa kurejea nyumbani haraka. Tangu kuingia madarakani Januari 20, mwaka huu, Trump amelumbana na vyombo vya habari kwa namna mbili. Mosi; amelumbana navyo yeye moja kwa moja katika moja ya mkutano wake na vyombo hivyo ambapo aliwaita waandishi feki. Pili; kwa sasa anawatumia wasaidizi wake ambao wameonyesha msimamo mkali wa kiongozi huyo katika malumbano hayo. Uhusiano wa vyombo vya habari na Trump ulikuwa mbaya tangu alipoanza mchakato wa kuwania urais ndani ya chama chake. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Habari, Sean Spicer, vyombo vya habari vinaandika habari mbaya dhidi ya Trump hususani juu ya idadi ndogo ya watu waliojitokeza siku ya kuapishwa kwake. Naye mshauri wa Ikulu, Kellyanne Conway, ameunga mkono hatua hiyo na kudai Spicer alizungumza ukweli. Wawili hao wanadai Trump hatendewi haki na vyombo vya habari. Kwa upande wake Katibu Mkuu Kiongozi, Reince Priebus pamoja na Rudy Giulliani, wamevishutumu vyombo vya habari kuwa vinakosea kulinganisha idadi ndogo ya watu waliohudhuria wakati wa kuapishwa Trump na kipindi cha kuapishwa Obama mwaka 2009, wakidai kuwa wingi au uchache wa watu si jambo lenye umuhimu. Serikali ya Trump imetangaza kuwa itasaini upya mkataba wa kibiashara kwa nchi za Amerika Kaskazini. Mkataba wa NAFTA (North America Free Trade Agreement), unazihusisha pia nchi za Canada na Mexico, Trump amebainisha kuwa anazingatia zaidi masuala mawili pekee kati ya mengi; suala la uhamiaji na ulinzi mipakani. Anataka mkataba huo uwe na manufaa kwa Marekani badala ya kubeba mzigo wa wengine: Tutakutana na Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau na vile vile Rais wa Mexico, Pena Enrique Nieto. Tutasaini mkataba katika masuala hayo,” ilisema taarifa ya Trump. Uhusiano wa Marekani na Israel una historia ndefu. Rais mpya ameonekana kuwa na mtazamo mpya na tayari kuna madai ya kuhamisha ubalozi wa Marekani nchini Israel kutoka mjini Tel Aviv kwenda mji wa Jerusalem. Suala hilo ni miongoni mwa mambo yaliyozua mjadala mkali miongoni mwa mataifa ya bara la Asia yakipinga wazi mpango huo. Kiongozi wa Mamlaka ya Palestina, Mahmood Abbas na Mfalme wa Jordan, Abdullah II wanapinga mpango huo. Wanasema unaweza kusababisha machafuko mapya katika eneo la Mashariki ya Kati. Tangu kuingia madarakani amefanya ziara ya kwanza katika Ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Kijasusi nchini Marekani, CIA. Pamoja na mambo mengine, Trump ametangaza kumteua Mike Pompeo kuwa Mkurugenzi wa CIA. Kabla ya uteuzi huo, Pompeo alikuwa mbunge wa Baraza la Wawakilishi wa Jimbo la Kansas tangu mwaka 2011 hadi 2017. Trump ametangaza kufuta mpango wa kutoa misaada kwa asasi zinazojihusisha na harakati za kuunga mkono utoaji mimba. Trump amefuata nyayo za Ronald Reagan kupiga marufuku utoaji mimba uliopo chini ya sheria ya ‘Gag rule’ kama sehemu ya sera ya MCP (The Mexico City Policy) iliyokuwa ikipiga marufuku kufadhili utoaji mimba duniani mwaka 1984.  Ilianza kutumika katika utawala wa Reagan mwaka 1984 na baadaye George W. Bush ambao walisababisha kiwango cha utoaji mimba kuwa kikubwa nchini Marekani. Tangu mwaka 1973 chini ya Sheria ya Helms Amendment, ni makosa kutumia fedha za Serikali kushughulikia masuala ya utoaji mimba popote duniani. Hatua hiyo inatajwa kuziathiri asasi mbalimbali na kusababisha ukata mkubwa miongoni mwake. Serikali ya Trump inaundwa na baraza la mawaziri dogo mno wapo 21 tu. Uteuzi wa mawaziri ulikamilika Januari 12, mwaka huu. Licha ya kuteua zaidi ya maofisa 4,000 katika nafasi mbalimbali, Trump anakabiliwa na mtihani wa kukubaliwa wateule wake 1,100 wanaotakiwa kuidhinishwa na Bunge la Seneti. Kati ya wateule wake 450 wanatajwa kutokuwa na sifa zinazotakiwa na Bunge la Seneti. Katika utawala wa Rais Mstaafu Barack Obama, alifanikiwa kupitisha sheria ya kuwatambua na kuwapa haki watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja maarufu kama mashoga na wasagaji. Nilimsikiliza Rais wa Mexico, Pena Nieto, alipozungumza na Televisheni ya Africa News Jumanne wiki hii kuhusu mkataba wa TPP (Trans-Pacific Partnership). Nieto alikuwa akizungumza huku amekunja sura na kuonyesha ishara kuwa rais huyo ameumizwa na uamuzi wa Serikali ya Trump kujitoa kwenye mkataba wa kibiashara wa kanda ya Pasifiki unaojumuisha nchi 12 za Mexico, Canada, Peru, Vietnam, Malaysia, Brunei, Japan, New Zealand, Singapore. Licha ya uamuzi huo, mataifa mengine yamesema yatasonga mbele. Trump amezungumza na Rais wa Misri, Abdel Fattah Al-Sisi kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili ikiwamo kupambana na ugaidi. Al Sisi ni kiongozi pekee kutoka Afrika ambaye amepewa nafasi ya kwanza kuzungumza na Trump. Haijulikani itakuwaje kwa wengine. Kiongozi huyo ametoa mwongozo wa kufutwa ajira zote serikalini isipokuwa kwa upande wa ajira za jeshini pekee. Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ndiye kiongozi wa kwanza kualikwa na Trump tangu alipoingia madarakani rasmi Januari 20. Kwa mujibu wa taarifa ya Televisheni ya Africa News, Israel na Marekani ni washirika wa muda mrefu, inatarajiwa watazungumzia suala la nyuklia ya Iran hali ambayo inasubiriwa kwa hamu kujua hatima ya mkataba wa nyuklia. Trump wakati akiwa kwenye kampeni, alikosoa mkataba huo na kudai angeufuta mara moja. Jumatano wiki hii, Trump alisaini hati ya kusitisha visa siku 30 kwa nchi za Sudan, Iran, Iraq, Libya, Somalia, Syria na Yemen. Hatua hiyo inatajwa kutekeleza sera zake za kuwapiga marufuku Waislamu kuingia nchini Marekani pamoja na kuanzisha daftari maalumu la kuwasajili. Suala la ujenzi wa ukuta mpakani mwa Mexico na Marekani limechukua sura mpya. Rais wa Mexico anapingana na mpango wa Trump na kudai anaingilia haki za taifa lake. Akizungumzia ujenzi wa ukuta kwenye mahojiano na Televisheni ya ABC nchini Marekani, Trump alisema: “Ujenzi unatarajiwa kuanza hivi karibuni haraka iwezekanavyo,… utajengwa tu. Naweza kusema kwa mwezi mmoja, … ndiyo! Ndani ya mwezi mmoja. Mipango inaanza karibuni. Yote yatafanyika kutokana na kile kitakachotokea Mexico. Tutaanza kwa makubaliano muhimu karibuni na yatafanyika kwa taratibu maalumu. Mexico watalipia gharama za ujenzi. Zitakuwa taratibu ngumu kidogo.” Kwa upande wake, Rais Nieto alijibu mapigo ya kauli hiyo kwa kusema: “Mexico haiamini katika ujenzi wa ukuta. Mara nyingi nimesema hayo, narudia tena, Mexico haitalipa gharama zozote za ujenzi wa ukuta. Tunaomba kuheshimiwa kama taifa huru. Mexico imekuwa rafiki wa watu wa Marekani na ina matumaini kutakuwa na makubaliano kati ya Serikali hizi. Makubaliano ambayo yatainufaisha Mexico na wananchi wake.” Hadi sasa marais hao wamefuta mkutano wao waliopanga kuufanya wiki ijayo. Taarifa ya kufutwa ilianza kutolewa na Rais Nieto ambaye alibainisha kuwa kutokana na uamuzi wa kujenga ukuta huo haoni sababu za kutembelea Washington. Naye Trump alijibu mapigo ya taarifa hiyo kwa kubainisha hakuna sababu za kukutana kwao tena. Saa chache tangu Bunge la Kongresi kuidhinisha jina la mteule wa Rais Trump katika wizara ya mambo ya nje wa Marekani, Rex Tillerson, ameshuhudia maofisa kadhaa wa Ikulu wakiachia ngazi hali ambayo inatajwa kuathiri mwelekeo wa sera za nje huku waziri huyo akikosa msaidizi. Waliojiuzulu ni Patrick Kennedy (aliyedumu kwa miaka tisa kama msaidizi wa waziri), Joyce Anne Barr (aliyekuwa ofisa utawala wa wizara hiyo), Michael Bond (mshauri wa mambo ya nje wa wizara), Balozi Gentry O. Smith (mkurugenzi wa wizara katika mipango ya nje). Makala haya yametayarishwa kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari.
2
KOCHA Mkuu wa timu ya Soka ya Taifa, Taifa Stars, Etienne Ndayi- ragije, ametangaza kikosi cha wachezaji 20 watakaoingia kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Sudan inayaotarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki hii. Katika kikosi hicho, kocha huyo wa muda amemwita Mzamiru Yas- sin wa Simba, ikiwa ni muda mrefu umepita tangu kuachwa kwenye kikosi cha Stars. Mechi hiyo ni ya kuwania fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani Chan, 2020. Wachezaji wengine walioitwa kikosini ni Juma Kaseja (KMC), Metacha Mnata (Yanga ), Saidi Kipao (Kagera Sugar), Haruna Shamte, Mohammed Hussein, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Hassan Dilunga, Miraji Athumani, Mzamiru Yassin na Gadiel Michael (Simba). Kelvin Yondani, Mohammed Issa, Abdul Makame na Feisal Salum (Yanga), Iddi Seleman, Mudathir Yahya, Salum Abubakar, Frank Domayo na Shaaban Chilunda (Azam). Wengien ni Ayoub Lyanga, Ba- kari Nondo kutoka Coastal Union, Iddi Mobi na Baraka Majogoro kutoka Polisi Tanzania na Boniface Maganga wa KMC. Kikosi hicho kilitarajiwa kuingia kambini jana. Mshindi wa mechi hiyo itakayochezwa nyumbani na ugenini atafuzu hatua ya makundi.
4
SERIKALI imezitaka hospitali na vituo vya afya nchini kutumia runinga zao kutoa elimu ya afya tu huku ikisema kuwa elimu hiyo itaanza kutolewa pia katika mabasi yaendayo mikoani.Agizo hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile mwishoni mwa wiki.Ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kujua hali ya upatikanaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Benjamini Mkapa jijini Dodoma.Amesisitiza hayo alipozungumza maadhimisho ya magonjwa ya moyo duniani ambapo Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dar es Salaam iliafanyia Hospitali ya Vijibweni, Kigamboni. Alisema serikali inaamini njia nzuri kutokomeza magonjwa yasiyoambukiza ni kutoa elimu.Alisema serikali imeelekeza televisheni zote katika hospitali na vituo vya afya zisioneshe vipindi vya mipira, muziki wala filamu. Badala yake, aliagiza zitoe elimu juu ya magonjwa mbalimbali na huduma za afya ambapo waraka huo umesambazwa nchi nzima.“Hapa nasisitiza tu lakini tayari tulishasambaza waraka. Lakini pia tunafanya mazungumzo na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) ili kwenye mabasi ya abiria kwenda mikoani pamoja na mambo mengine watakayoonesha kuwe na mapumziko ya muda kutoa elimu ya afya,” amesema Waziri Ndugulile.Amesema serikali imeshaandaa CD zenye vipindi vya afya kuhakikisha zinagawiwa nchi nzima ili umma upewe elimu ya magonjwa mbalimbali.Amesema serikali inaamini njia bora kukabiliana na magonjwa ni kuyakinga hivyo ina mpango wa kuanzisha mkakati wa kitaifa wa magonjwa yasiyoambukiza na kushusha tiba mpaka katika hospitali na vituo vya afya kuokoa gharama za wagonjwa kusafiri kufuata huduma mbali.“Kwa sasa serikali inaboresha sana huduma za matibabu ya moyo kupitia JKCI na kushusha zaidi huduma hizi hospitali za kanda kwa kufunga vifaa vya kisasa. Sasa tunaweza kupima na kutibu kwa njia za kisasa,” amesema.Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo JKCI, Delila Kimambo alisema bado watu wengi wana matatizo ya shinikizo la juu la damu (BP) lakini huwa hawafahamu kuwa wana tatizo hilo.Amesema wengine wanafahamu wana tatizo hilo lakini hawatumii dawa kwa mpangilio unaofaa.Amesema JKCI katika kuadhimisha siku hiyo juzi ilitoa huduma ya wananchi kupima ugonjwa huo bure na kutoa ushauri katika kushiriki nao maadhimisho ya siku hiyo dunia nzima yakiwa na kauli mbiu ‘moyo wangu, moyo wangu’.Amesema JKCI walifanya maadhimisho hayo Kigamboni kuwafuata wananchi hasa ambao hawana uwezo wa kufika JKCI kupima afya.Mbali na moyo pia wananchi walipima sukari. Imeandikwa na Anastazia Anyimike, Dodoma na Regina Kumba Dar.
3
SHERIA mpya ya uwezeshaji wa biashara inaandaliwa ikitarajiwa kuja na majibu kuhusu utekelezaji wa maboresho ya mfumo wa udhibiti wa biashara.Aidha, mikoa yote na mamlaka na taasisi za serikali kutenga muda maalumu wa kutatua kero na changamoto zinazokabili wawekezaji wakati mawaziri kadhaa wakifanya ziara kwa kazi hiyo ya kusikiliza kero za wawekezaji kutokana na agizo la Waziri Mkuu.Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki alisema aidha serikali inaendelea kufanya marekebisho ya sera ya uwekezaji ambayo ni ya muda mrefu tangu mwaka 1996.Kairuki alisema hayo juzi kwenye ufunguzi wa kongamano la fursa za biashara na uwekezaji la mkoa wa Pwani lililofunguliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.“Tunakuja na sheria nyingine mpya itakaoitwa Sheria ya Uwezeshaji wa Biashara ambayo kimsingi ndiyo itafanya utekelezaji wa yaliyoelekezwa kwenye blue print ili kufanya kwa haraka zaidi,” alisema Kairuki akimkaribisha waziri mkuu.Waziri Kairuki alikuwa akizungumzia dhamira ya serikali katika kutatua changamoto za uwekezaji nchini kulingana na maelekezo ya viongozi wa juu. Wakati huo huo waziri Kairuki ameagiza mikoa yote na mamlaka na taasisi za serikali kutenga muda maalumu wa kutatua kero na changamoto zinazokabili wawekezaji katika shughuli zao. Alisema kwa maelekezo ya Waziri Mkuu, pia mawaziri akiwamo wa Wizara ya Nishati, wameanza kazi ya kutembelea mikoa.Wameshafanya hivyo kwa mikoa minne ziara inayohusisha mawaziri takribani saba wanaosikiliza kero za wawekezaji. Wanaendelea pia kukutana na wawekezaji wa kigeni kupitia chemba zao pamoja na balozi.
3
*Kadi huenda zikaigharimu kukosa wachezaji tegemeo *Wakacha kambi ya Uturuki, kutua leo Dar NA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM WAWAKILISHI wa kimataifa klabu ya soka ya Yanga, wanaweza kujikuta katika wakati mgumu kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, kama watashindwa kufanyia kazi suala la nidhamu ndani ya uwanja. Hatua hiyo inatokana na kitendo cha wachezaji watano wa timu hiyo, Donald Ngoma, Haruna Nyonzima, Simon Msuva, Amissi Tambwe, kupewa kadi za njano huku beki, Haji Mwinyi, akipewa  kadi nyekundu kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi A uliochezwa juzi dhidi ya Mo Bejaia kwenye Uwanja wa Unite Maghrebine mijini, Bejaia, Algeria. Hata hivyo, mchezo huo ulimalizika kwa Yanga kukubali kichapo cha 1-0, hivyo kuifanya timu hiyo kuanza vibaya hatua ya makundi ya michuano hiyo. Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Mkurugenzi wa Mashindano Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jonas Kiwia, alisema kadi hizo za njano zinaweza kuiathiri timu kwenye mchezo ujao, ambapo Juni 28 mwaka huu timu hiyo itacheza na timu ya TP Mazembe, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. “Sina uhakika kama kuna adhabu nyingine ambayo klabu hiyo inaweza kupewa kutokana na kadi hizi, lakini ninavyofahamu inaweza kutokea kwa mchezaji mmoja mmoja kama kadi hizo zitaongezeka na kufikia mbili anaweza kukosa mchezo unaofuata. “Kitendo hicho ambacho sababu yake ni utovu wa nidhamu uwanjani, kinaweza kuigharimu timu kwa kukosa wachezaji tegemeo kutokana na adhabu kama hiyo,” alisema Kiwia. Naye Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro, alisema wamekubali matokeo ya mchezo huo na kuwatoa hofu mashabiki wake kwa kudai kwamba kufungwa katika mchezo huo si sababu ya wao kupoteza matumaini ya kufanya vema mbeleni. “Tumekubaliana na matokeo sasa tunajipanga kuangalia wapi tulikosea, tumeanza robo fainali kwa kufungwa lakini hii isituvunje moyo kwani sisi tuna kawaida moja, huwa tukianza na kufungwa basi tunamalizia kwa ushindi, hivyo nawaambia mashabiki Yanga bado ipo kamili,” alisema. Jerry alisema licha ya Yanga kufungwa katika mchezo huo, wachezaji walionyesha umahiri wa hali ya juu jambo alilosema kuwa hiyo imedhihirisha wazi kuwa timu hiyo kwa sasa ni moto wa kuotea mbali. Katika hatua nyingine, Jerry alisema timu hiyo itawasili mapema leo ikitokea nchini Algeria na itaendelea na kambi hapa jijini Dar es Salaam badala ya kurudi tena Uturuki kama ilivyopangwa hapo awali.
4
NA ZAINAB IDDY, DAR ES SALAAM BABA mzazi wa kipa namba moja wa timu ya Mbeya City, Abdallah David, amemzuia mwanaye David Burhani, kuichezea timu hiyo kwa kile alichodai kupotezewa muda na timu hiyo. Burhani alisimamishwa kwa muda usiojulikana na uongozi wa timu hiyo, siku chache baada ya kudaiwa kuihujumu timu hiyo katika mchezo wao dhidi ya Yanga. Katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Sokoine mjini humo, Yanga walishinda mabao 3-1 huku Burhani akidaiwa kufanya uzembe wa kuruhusu kufungwa bao la pili na mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa. Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi, Burhani alisema kuwa hana mpango wa kuendelea kuitumikia Mbeya City na hiyo imetokana na baba yake kumtaka aachane nayo kwa kuwa imeonekana kuendeshwa kwa fitina. Alisema baba yake alimtaka kutafuta nafasi ya kucheza sehemu nyingine hata kwenye klabu zisizoshiriki Ligi Kuu ili kuendeleza kipaji chake na yeye hakuona ubaya kwa kuwa mkataba wake unamruhusu kufanya mazungumzo na timu yoyote. “Kutokana na hali iliyojitokeza, baba amenishauri kutoendelea na Mbeya City, kwani inaonekana kuna watu wachache wenye mamlaka ya kutoa maamuzi kulingana na matakwa yao na si kwaajili ya maendeleo ya timu. “Sikuona ubaya ushauri wa baba yangu na katika hilo nimeanza mazungumzo na timu kutoka nje ya nchi ambazo zinapakana na Mkoa wa Mbeya, kama mambo yakienda vizuri kuna uwezekano nikaondoka na kwenda kuanza maisha mapya,” alisema. Akizungumzia juu ya suala lake na uongozi wa Mbeya City, Burhani alisema kuwa hadi sasa hajapokea taarifa yoyote kutoka kwa uongozi wa timu hiyo. “Waliniambia wanafanya uchunguzi tuhuma zinazonikabili hivyo nitakuwa nje hadi watakapokamilisha suala lao, lakini hadi sasa sijapokea taarifa yoyote kutoka kwao name sioni umuhimu wa kuwauliza,” alisema.
4
KIUNGO wa Manchester United, Nemanja Matic, ameweka wazi kuwa, wana wachezaji wazuri vijana, lakini kutokana na kukosa uzoefu ubingwa wa Ligi Kuu msimu ujao watausikia kwa wengine. Mchezaji huyo anaamini kikosi hicho cha kocha Ole Gunnar Solskjaer, kinahitaji wachezaji wenye uzoefi mkubwa ili kuleta ushindani katika mbio za kuwania ubingwa. Matic mwenye umri wa miaka 30, anatajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wenye nafasi kubwa ya kupewa unahodha katika msimu mpya wa ligi. Katika michezo ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya mchezaji huyo amecheza michezo yote ya ushindi dhidi ya Perth Glory, Leeds, Inter Milan na Tottenham. “Wachezaji bora na wenye uzoefu wanaweza kukupa taji, kwenye kikosi chetu tuna wachezaji wengi wazuri, lakini hawana uzoefu. “Tuna wachezaji watano au sita wenye uwezo mkubwa, ila bado ni vijana kama vile Marcus Rashford na Anthony Martial. Wamekuwa kwenye kiwango cha hali ya juu, lakini bado hawana mchango wa kuweza kuipa timu ubingwa. “Mason Greenwood ni faida ya baadae, najua Man United wapo kwenye mipango ya baadae kwa wachezaji waliowasajili, lakini wanatakiwa kupewa muda kwa kuwa ukiwa na miaka 17 hawezi kufanya kama mtu mwenye umri wa miaka 26 au 27. “Siku zote soka linahitaji matokeo, lakini mashabiki wanatakiwa kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki ninaamini kwa wachezaji waliopo wanaweza kuifanya Man United kurudi kwenye heshima yake hapo baadae,” alisema mchezaji huyo. Kiungo huyo mkabaji raia wa nchini Serbia, ana uzoefu mkubwa na Ligi ya England, alikuwa miongoni mwa wachezaji waliochukua Ligi Kuu England mwaka 2015 na 2017 katika kikosi cha Chelsea kabla ya kujiunga na Man United. Ligi Kuu England inatarajiwa kuanza Agosti 9 mwaka huu huku Manchester United wakishuka dimbani Agosti 11 dhidi ya Chelsea kwenye mchezo wao wa ufunguzi ambao utapigwa kwenye uwanja wa Old Trafford.
4
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema hakuna Mtanzania yeyote ambaye simu yake itazuiwa kutumika, kwa sababu hajasajili, kwa kigezo cha kutokuwa na Kitambulisho cha Taifa.Kwa maana hiyo, ikifika Desemba 31 mwaka huu, ambayo ni mwisho wa kusajili laini za simu kama mtu hajapata kitambulisho cha taifa, laini yake ya simu haitazimwa na ataendelea kuitumia.Aidha, Lugola amemwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho Vya Taifa (NIDA), kuhakikisha kwamba maofisa wa NIDA wilaya zote, wanapeleka namba za vitambulisho vijijini ; na si kutegemea kuzipata katika simu.Lugola alitoa maelekezo hayo jana bungeni na wakati akijibu mwongozo wa Mbunge wa Kavuu, Dk Pudenciana Kikwembe (CCM), ambaye katika mwongozo wake alisema uandikishaji wa vitambulisho vya taifa, umekuwa na changamoto maeneo ya vijijini. Alisema kuwa tatizo hilo limekuwa kubwa hasa vijijini hususani majimbo ya Kavuu na Mlele, ambako uandikishaji umekuwa ni shida.“Kama inavyojulikana mwisho ni Desemba mwaka huu, naomba kujua kauli ya serikali nini kinafanyika ili waweze kupata vitambulisho,”alisema Pudenciana.Akijibu mwongozo huo, Lugola aliwatoa hofu wasiwasi Watanzania kuwa utaratibu wa utambuzi, usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wananchi, ambao wana sifa za kupata vitambulisho ni endelevu.“Zoezi hili halina mwisho wala halina tarehe kwamba ikifika tarehe fulani kuna Mtanzania hajapata kitambulisho, basi huyo Mtanzania hatapata kitambulisho tena, Watanzania wasiwe na wasiwasi, hili ni zoezi endelevu na ndio maana kila mwaka kuna Watanzania ambao wanafikisha miaka 18.” alisema.Akizungumzia suala la usajili wa laini kwa vidole, Lugola alisema: “Naomba niwatoe wasiwasi Watanzania wote kwamba maelekezo Rais John Magufuli hakuna Mtanzania ambaye simu yake itazuiwa kutumika eti kwa sababu hana kitambulisho cha taifa na hivyo hajasajili laini yake.”Alisema kuwa lengo la usajili na utambuzi, ilikuwa wananchi milioni 23.3, lakini hadi sasa wamesajili watanzania milioni 20.5 na wamezalisha namba za vitambulisho kwa watanzania milioni 15.5.Kwa mujibu wa mtandao wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), hadi Juni mwaka huu laini zilizokuwa zinatumika ni 43,749,086.“Utaratibu wetu ni kwamba hapa Mtanzania ambaye hajapata kitambulisho, atumie namba yake ya utambulisho. Nitoe agizo sasa kwa Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, maofisa wa NIDA wahakikishe hizi namba ambazo zimeshazalishwa wazipeleke kwa wenyewe kule vijijini, tusitegee masuala ya kuzipata katika simu” alisema.Alisema wakishapeleka namba hizo, kila mwenye namba asaini kuwa amepata. Pia, aliwaagiza wakuu wa wilaya, kuhakikisha wanapata taarifa kutoka NIDA kuwa tayari kila mtanzania amepata namba ya taifa ili akimbizane na usajili wa laini.Gazeti hili lilipomtafuta Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe kuhusu tangazo hilo la Lugola kuwa ifikapo Desemba 31, mwaka huu hakuna laini ya simu itakayozimwa kutokana na kutosajiliwa kwa kukosa Kitambulisho cha Taifa, alimtaka mwandishi amuulize aliyetoa taaifa hiyo(Lugola).Kamwelwe alisema kama mwandishi anataka majibu ya Wizara yake(Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), aandike maswali kimaandishi ili ajibiwe kimaandishi.
3
['Timu ya kandanda ya taifa Stars kutoka tanzania imeiondoa timu ya harambee Stars kutoka kenya katika mashindano ya CHAN 2020', 'Timu ya Kenya Harambee Stars ilidondoka katika michuano ya kufuzu kombe la CHAN 2020 baada ya kupoteza kwa Tanzania taifa Stars 4-1 kupitia mikwaju ya penalti katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi baada ya kutoka sare 0-0 katika dakika 90 za mchezo. ', 'Mkufunzi wa Harambee Sebastien Migne alichagua washambulia waliokuwa na kasi akiwemo Samuel Onyango na Duke Abuya lakini hawakuweza kucheka na wavu, na ilipofikia majira ya penalti Taifa Stars ilithibitisha kwamba wao ndio magwiji watakaoelekea Camroon ambapo michuano hiyo itachezwa mwezi Januari.', 'Harambee Stars walikuwa wametoka sare ya 0-0 siku ya Jumapili iliopita mjini Dar es Salaam na kufuatia ushindi huo Taifa Stars sasa itakutana na Sudan katika raundi ya pili na ya mwisho ya kufuzu.', 'Safu ya mashambulizi ya Harambee Stars ilionyesha ukakamavu wa mashambulizi lakini hawakuweza kufua dafu mbele ya safu ya ulinzi iliowekwa na Taifa Stars. ', 'Joash Onyango alionyesha umahiri wake katika safu ya ulinzi ya Kenya na kuzuia hatari iliokuwa ikisababishwa na Jonas Mkudde.', 'Safu ya mashambulizi ya Harambee Stars ilionyesha ukakamavu wa mashambulizi lakini hawakuweza kufua dafu mbele ya safu ya ulinzi iliowekwa na Taifa Stars. ', 'Joash Onyango alionyesha umahiri wake katika safu ya ulinzi ya Kenya na kuzuia hatari iliokuwa ikisababishwa na Jonas Mkudde.', 'Iddi Alli alikosa bao la wazi kufuatia uvamizi wa Taifa Stars katika lango la Kenya baada ya Isuza kupokonywa mpira.', 'Kipindi cha kwanza kiliisha kwa sare tasa lakini Harambee Stars ilikaribia kufunga katika kipindi cha pili baada ya Miheso wa Kenya kuvamia lango la taifa Stars.', 'Tanzania ilikaribia kufunga kupitia mshambuliaji wake Mkudde lakini ulinzi mzuri wa Miheso ulimzuia mshambuliaji huyo matata.', 'Kunako dakika za mwisho Mkudde alivamia tena lango la Harambee Stars baada ya kumpokonya mpira Oyemba wa Kenya na kusalia na goli lakini mshambuliaji huyo mrefu wa Tanazania akapiga nje.']
4
KATIKA kuunga mkono sera ya serikali ya kukuza viwanda sambamba na kuwawezesha wananchi kiuchumi, kampuni inayozalisha vinywaji jamii ya soda ya Watercom imetoa ajira kwa wananchi zaidi ya 3000 wanaofanya kazi ya uzalishaji na usambazaji wa bidhaa zinazozalishwa na kampuni hiyo.Aidha, pamoja na ajira hizo, kampuni hiyo pia imeviwezesha kimitaji vikundi 300 vya wajasiriamali vikiwemo 40 vya jijini Dar es Salaam ili waweze kutimiza ndoto zao za kibiashara na hivyo kujinasua kutokana na tatizo la umasikini linalozikabili familia nyingi nchini na dunia kwa ujumla.Akizungumza wakati wa uzinduzi wa vinywaji hivyo Jijini Dar es Salaam jana, Meneja Mauzo wa kampuni hiyo Shiraz Batchu, alisema ujio wa bidhaa hizo zinazozalishwa kupitia uwekezaji uliofanywa na mzawa ni hatua iliyolenga kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli kuanzisha na kuendeleza viwanda hapa nchini.Alisema kampuni hiyo inayojihusisha na uzalishaji wa maji aina ya afya, pamoja na kinywaji hicho imekuja na vinywaji jamii ya soda ambavyo kimsingi vyote vimelenga kunyanyua soko la ndani na nje ya nchi sambamba na kutoa ajira kwa makundi mbalimbali ya wananchi.“Kupitia viwanda vyetu mbalimbali kikiwemo kinachozalisha bidhaa hii mpya ya soda, tumeweza kutoa ajira kwa wananchi mbalimbali pamoja na kuviwezesha kiuchumi vikundi vya akina mama kwa kuvipa mitaji ambayo kimsingi imewasaidia katika kupambana na umasikini,” alisema Batchu.Alisema kampuni hiyo inayomiliki pia kiwanda cha maziwa cha maarufu kama Dar Fresh, pamoja na kampuni ya mafuta jamii ya Petrol ya Oilcom, imekuja na kinywaji cha kusisimua misuli kiitwacho ‘jembe’ na Turbo ambavyo humsaidia mtumiaji kuondoa uchovu mwilini” alisema Batchu.Aidha alisema ukiacha ajira rasmi 3000 zilizotolewa na kampuni hiyo, pia kuna ajira zingine zisizo za moja kwa moja kwa wafanyakazi 300,000 wakiwemo wauzaji na wasambazaji wa bidhaa hizo waliopo maeneo mbalimbali nchini, hatua aliyoidai kuwa kwa kiasi fulani imesaidia kutatua tatizo la ajira kwa vijana wengi nchini. Aidha aliwataka wananchi hususani vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli za kuliletea maendeleo Taifa ili kufikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo 2025.
3
Na AZIZA MASOUD- DAR ES SALAAM TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vya siasa kufuata taratibu za kisheria endapo ukiukwaji wa maadili ya uchaguzi utatokea katika kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea nchini ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhani Kailima, baada ya Chama cha ACT-Wazalendo kuwataja watendaji wa Serikali ya Kata ya Nkome mkoani Geita kuwaandikisha wazee ili kuwapatia huduma za afya bure wakiwa na kadi za kupigia kura kinyume na taratibu za uchaguzi. Kailima alisema NEC imeyapata malalamiko hayo kupitia vyombo vya habari yanayoonyesha watendaji wa umma na vyombo vya dola kukipendelea Chama Cha Mapinduzi (CCM). “Kwa kuzingatia sehemu ya 5.4 ya Maadili ya Uchaguzi, NEC inavikumbusha vyama vya siasa kuwa iwapo vina malalamiko ya ukiukwaji wa maadili ya uchaguzi katika uchaguzi mdogo wa udiwani kuwasilisha malalamiko hayo katika kamati ya maadili ya kata saa 72 tangu ukiukwaji huo umefanyika,” alisema. Kailima alisema endapo chama cha siasa au mgombea wa nafasi husika katika kampeni za uchaguzi mdogo anaamini maadili ya uchaguzi yamekiukwa awasilishe malalamiko yake katika kamati ya maadili ya ngazi husika. “Hivyo tunakishauri ACT na vyama vingine kuwasilisha malalamiko ya ukiukwaji wa maadili katika kamati husika,” alisema. Pia alisema kwa kuzingatia sehemu ya 5.7(a) ya maadili ya uchaguzi, endapo mgombea au chama atakuwa hajaridhishwa na uamuzi wa kamati ya maadili ya ngazi ya kata anaweza kuwasilisha malalamiko yake katika ngazi ya msimamizi wa jimbo. Alisema malalamiko hayo yanapaswa kuwasilishwa ndani ya saa 24 baada ya uamuzi wa kamati ya kata kutolewa. Alisema endapo chama kitakuwa hakijaridhishwa na uamuzi wa ngazi ya jimbo wana uwezo wa kuwasilisha rufaa hiyo katika Kamati ya Maadili ngazi ya Taifa au rufaa ambazo ni NEC kwa kuzingatia sehemu ya 5.7(b) na (c). Alisema kwa mujibu wa sehemu ya 5.7(e) ya maadili ya uchaguzi, kama mgombea au chama atakuwa hajaridhishwa na uamuzi wa kamati ya rufaa atakuwa na fursa ya kuwasilisha malalamiko hayo mahakamani baada ya uchaguzi. Alisema malalamiko hayo yatawasilishwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi sura 343 na sheria ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa sura namba 292. Kailima pia alisema kwamba, ni kosa kumiliki kadi ya kura isiyokuwa yako chini ya kifungu cha 88 cha Sheria ya Taifa ya uchaguzi sura ya 292 kifungu cha 100 cha sheria ya uchaguzi ya Serikali za Mitaa sura ya 292. Aliwasihi wanasiasa na wadau wengine wa uchaguzi kuendelea na kampeni za kistaarabu za kuzingati sheria, kanuni na maadili ya uchaguzi kwa kuwa ofisi hiyo haitasita kuchukua hatua kwa mtu yeyote atakayekiuka.
3
 JESSCA NANGAWE– DAR ES SALAAM MABINGWA wa michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC), maarufu kwa Kombe la FA, timu ya Azam wanatarajiwa kukutana na Simba katika mchezo wa robo fainali. Katika droo iliyochezeshwa jana, jijini Dar es Salaam, Yanga watavaana Kagera Sugar, wakati Sahare All Stars wakimenyana na Ndanda huku timu ya Namungo itapepetana na Alliance. Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa timu ya Azam, Thabit Zakaria ‘Zaka za Kazi’, alisema mara baada ya droo hiyo kikosi chao kitaendelea kujifua vyema kwa kuwa kina kazi kubwa ya kufanya ikiwamo kutetea taji hilo kwa mara nyingine ili waweze kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika. “Kwa sasa timu upo kwenye maandalizi, kwanza tunajiandaa na Ligi Kuu Bara ambayo itarejea Juni 13, mwaka huu, baada ya kusimama mzunguko wa 29 kutokana na hofu ya kuenea kwa maambukizi ya virusi vya corona,” “Malengo yetu ni kuona tunatetea ubingwa wetu wa Kombe la Azam kwa mara nyingine ili tuendelee kuiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa,” alisema Zaka za Kazi.
4
RAIS John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Apson Mwang’onda (pichani), Ikulu jijini Dar es Salaam.Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jana ilisema baada ya mazungumzo hayo Mwang’onda alimshukuru Rais Magufuli kwa kukubali ombi lake la kumuona na kuzungumza naye. Pia alimpongeza kwa uongozi mzuri unaochochea kasi ya maendeleo hususani katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo.Mwang’onda aliitaja baadhi ya miradi mikubwa ya maendeleo kuwa ni mradi wa uzalishaji wa umeme katika mto Rufiji (Stieglers’ Gorge) na ujenzi wa madaraja na barabara ambazo licha ya kurahisisha usafiri zitasaidia kuondoa msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam.“Mabadiliko ni makubwa sana ambayo yametokea, kuna miradi mikubwa mingi inafanyika sasa hivi, kwa hiyo mabadiliko ni makubwa kusema kweli na yote hayo ni kwa manufaa ya nchi, kwa hiyo nachoweza kusema amefanya kazi kubwa kwa maendeleo ya nchi” alisema Mwang’onda. Alitoa mwito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Awamu ya Tano ili itekeleza mipango yake kwa ufanisi na kwa manufaa ya Taifa.
3
MAAFANDE wa Kikosi Cha Kuzuia Magendo (KMKM) wanashuka dimbani leo kucheza mchezo wa Ngao ya Hisani na timu ya Malindi. Mchezo huo ambao unaashiria kuanza kwa Ligi Kuu ya Zanzibar, utapigwa kwenye Uwanja wa Amaan na umekuwa na hisia kali kutokana na makocha wa pande zote kujiandaa kwa ushindi. Kocha wa KMKM, Ame Msimu alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanashinda mchezo huo. “Kiujumla, tumejipanga vizuri na mchezo wetu wa kesho (leo), pia ni mchezo wetu wa awali wa ngao ya jamii ari na hamasa yetu ni kuona tunashinda,” alisema. Kwa upande wa kocha wa makipa wa Malindi, Saleh Ahmed Machupa alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanarejesha heshima yao. Alisema, kuwa wao wamejipanga kwa ajili ya ligi yote, lakini kupitia mchezo huo wanataka kuhakikisha wanashinda na kuchukuwa ngao hiyo. “Tumejipanga kuhakikisha tunarejesha heshima ya Malindi kuchukua hii ngao na vikombe vilokuwepo mbele yetu”, alisema Machupa. Kabla ya mechi hiyo uwanjani hapo kutatanguliwa na mechi ya timu za vijana za Malindi na KMKM saa nane mchana.
4
WASHINGTON, MAREKANI MWANAMITINDO, Ivanka Trump, amejiunga rasmi na Serikali ya baba yake ambapo atahudumu kama mfanyakazi asiyelipwa, kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani, White House jana. Hatua hiyo inakuja baada ya wataalamu wa maadili kuhoji na kukosoa mpango wa awali wa binti huyo wa Rais Donald Trump wa kutaka kuhudumu katika wadhifa usio rasmi. Ivanka (35), ambaye cheo chake rasmi kinakuwa msaidizi wa rais, amesema amesikia ‘maswali ambayo baadhi ya watu walikuwa wakihoji kuhusu hatua yake ya kumshauri rais katika nafasi yake kama mtu binafsi. Mumewe, Jared Kushner, tayari ni mshauri mwandamizi wa Rais Trump. Kupitia taarifa yake White House imesema ina furaha kuwa Ivanka Trump amechukua hatua hii isiyotarajiwa katika nafasi yake kama binti wa rais. Trump alisema kupitia taarifa yake  amekuwa akifanya kazi kwa nia njema na kundi la washauri wa Rais Ikulu pamoja na mshauri wake binafsi kujadili kuhusu jukumu lake. Wataalamu kuhusu maadili walilalamika ilipobainika wiki iliyopita kuwa Trump angepewa ofisi White House pamoja na kibali cha usalama cha kuingia na kutoka Ikulu hiyo ilihali si sehemu ya wahudumu wa rais. Wakosoaji walisema kazi ya  Trump inapaswa kufanywa rasmi ndipo aweze kudhibitiwa na sheria kuhusu uwazi wa maafisa wa serikali pamoja na maadili. Aidha, adhibitiwe na sheria kuhusu mgongano wa maslahi. Wakili wa Trump, Jamie Gorelick, alisema mteja wake atawasilisha nyaraka stahili za kufichua utajiri wake kwa mujibu wa sheria kuhusu maadili ya watumishi wa umma Marekani.
2
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imewafi kisha mahakamani raia wawili wa China na Mtanzania mmoja, kwa tuhuma nne tofauti zikiwemo kujenga mtambo wa kusafi sha mafuta ya dizeli bila kuwa na kibali pamoja na kughushi cheti cha ukaguzi wa mazingira.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Takukuru, Ali Mfuru aliwataja raia hao wa China kuwa ni Yu Hattao na Zhang Zhi Xin ambao wanamiliki Kampuni ya SHIN UP (T) Ltd iliyopo Visiga Kibaha mkoani Pwani na Mtanzania mfanyabiashara ni John Mnyele.Mfuru alisema mshtakiwa wa kwanza Hattao anakabiliwa na makosa mawili, kosa la kwanza ni kughushi na kosa la pili ni kufanya kazi nchini bila kuwa na kibali.Aidha Mnyele anakabiliwa na kosa la kughushi cheti cha ukaguzi wa mazingira ili kuonesha kampuni hiyo imekaguliwa jambo ambalo sio kweli.Aidha makosa mengine ambayo yanawakabili washtakiwa wote watatu ni kuendesha shuhguli za ujenzi bila kuwa na kibali cha ukaguzi wa mazingira kinyume na kifungu cha Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake za mwaka 2005 na kifungu cha 60 (1) vikisomwa kwa pamoja na kifungu namba 191 cha Sheria ya Mazingira.Mfuru alisema makosa mengine kujenga mtambo wa kusafisha mafuta aina ya dizeli bila kuwa na kibali cha Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA),kinyume na kifungu cha 121 (1) na (2) cha Sheria ya Petroli namba 21 ya mwaka 2015.Kaimu Mkurugenzi huyo alisema watuhumiwa hao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana na kuwaomba watanzania wazalendo kuelendea kushirikiana na taasisi hizo katika kufichua watu wanaohujumu nchi na kujihususha na uhalifu na makosa ya rushwa.“Takukuru kwa kushirikiana na Polisi tunapenda kuwashukuru wananchi wazalendo wamekuwa mstari wa mbele kushirikiana na taasisi hizi katika kuwafichua wale wote wanaolihujumu taifa letu pamoja na kujihusisha na vitndo vya uhalifu na rushwa,”alisema Mfuru.Katika hatua nyingine,Takukuru imekanusha habari zilizochapishwa na gazeti moja la kila wiki inayosema ‘Takukuru wamalizana kiaina na mtuhumiwa’ na kusema habari haina ukweli kwani tukio hilo linaendelea kuchunguzwa kwa ushirikiana na vyombo vingine vya serikali vyenye mamlaka ya kufanya tathmini ya masuala yote ya kodi.
3
*Vijana wa miaka 20 hadi 40, waathirika wakubwa *Utafiti wa Ocean Road 2008, alisema 90 kansa ya koo wanaume, asilimia 10 wanawake. *Ocean Road kuna ongezeko la wagonjwa wa saratani ya koo 511 ndani ya kipindi cha miaka 12. *Mama mwenye virusi vinavyosababisha saratani hiyo akijifungua anaweza kumuweka mtoto kwenye hatari VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM IKIWA wewe ni miongoni mwa watu wanaopenda kushiriki mapenzi kwa njia ya mdomo (kunyonya sehemu za siri za mwezi wako), unapaswa kutambua kwamba unajiweka kwenye hatari ya kuishia kupata saratani ya koo. Akizungumza na MTANZANIA katika mahojiano maalumu hivi karibuni, Daktari Bingwa wa Idara ya Upasuaji wa Magonjwa ya Masikio, Pua, Koo na Vivimbe vya Kichwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Tawi la Mloganzila (MAMC), Godwin Mfuko, alifafanua kwa kina juu ya suala hilo. Alisema watu wanaojihusisha na ngono kwa njia hiyo wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa uitwao kitaalamu Recurrent Laryngeal papillomatosis (RLP). “Hii ni aina nyingine ya ugonjwa ambao unafanana na saratani, lakini si saratani moja kwa moja, unaweza kugeuka kuwa saratani ikiwa mtu hatapata matibabu yanayostahili kwa wakati. “Yaani unakuta kuna vivimbe vingi vimeota kooni, lakini vyenyewe si saratani, vivimbe hivyo hukaa kama mfano wa vioto (majani) pale kooni na hivyo kumfanya mhusika ashindwe kupumua vizuri. “Ikiwa mgonjwa hatapatiwa matibabu mapema, ile ‘infection’ (maambukizi) inaweza kupenya kwenye chembe chembe hai za mwili na hivyo kugeuka kuwa saratani, tunapokea watu wengi wanaougua ugonjwa huu hivi sasa,” alifafanua. Watoto nao waugua Bingwa huyo wa Mloganzila alisema katika kliniki zao wanapokea zaidi watoto kati ya miaka miwili hadi minne na vijana kuanzia umri wa miaka 20 hadi 40, wanaokabiliwa na ugonjwa huo. “Watoto hupata maambukizi kutoka kwa mama zao wakati wa kuzaliwa kwa njia ya kawaida, ikiwa mama ana maambukizi ya kirusi cha Human Papilloma (HPV) ukeni, huweza kumuambukiza mtoto wake wakati wa kujifungua,” alibainisha. Alisema kwa upande wa vijana wa miaka 20 hadi 40, katika kipindi hicho wanakuwa kwenye hatari ya kupata maambukizi hayo kwani ndicho kipindi ambacho wengi huanza kushiriki ngono.  “Ugonjwa huu hutokana na maambukizi ya kirusi hicho cha HPV ambacho hukaa sehemu za siri na ndicho ambacho husababisha saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake,” alibainisha. Wengi hutibiwa kama pumu Dk. Mfuko alisema watoto wengi wanaowapokea katika kliniki yao huwa wamepitia na kutibiwa kwenye hospitali mbalimbali kama wagonjwa wa pumu. “Nimeeleza awali kwamba, mtoto anakuwa kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu kama mama ana maambukizi ya HPV ukeni, anapozaliwa kwa njia ya kawaida. “Watoto wengi wanaokabiliwa na ugonjwa huu, dalili ya kwanza ambayo huonesha ni pale wanapofikisha umri wa miaka miwili, hushindwa kupumua vizuri, ndiyo maana utaona wengi hutibiwa kama pumu, lakini tunapowachunguza tunakuta wana vinyama vimeota kama majani kooni. “Majibu ya vipimo hutueleza wanaugua RLP, kwa kawaida vinyama hivyo vinavyokuwa vimeota, vinapokatwa huwa na tabia ya kuota tena, mgonjwa anaweza kufanyiwa upasuaji hata mara 30, unakuta vinajirudia kuota,” alisema. Alisisitiza kuwa kimsingi jamii inapaswa kuelewa kwamba, ngono kwa njia ya mdomo pekee (kunyonya sehemu za siri) hakusababishi mtu kupata saratani hiyo moja kwa moja. “Isipokuwa kuna huo uhusiano wa karibu na mtu anakuwa kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ikiwa huyo anayeshiriki naye ana maambukizi ya kirusi hicho cha HPV,” alisema. Alisema wapenzi wanaponyonyana sehemu za siri ikiwa mmoja ana maambukizi ya kirusi hicho, huingia kinywani na kwenda moja kwa moja katika chembe chembe hai za mwili. “Kwa hiyo ukiniuliza iwapo ngono kwa njia ya mdomo inasababisha saratani, nitakwambia hakuna jibu la moja kwa moja, kwa sababu mtu anaweza kupata maambukizi ya kirusi hiki lakini asipate saratani. “Atapata saratani ikiwa kirusi cha HPV kitaenda kuathiri chembechembe hai za mwili na kuingiza vinasaba vyake na hivyo kuzigeuza tabia yake na kuzifanya zikue bila mpangilio,” alifafanua. Kinachotokea “Hivyo, mtu akifanya ngono kwa njia hii hujiweka kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ya koo, kama yule anayemlamba anakuwa na maambukizi ya kirusi hiki. “Kwa sababu akipata maambukizi ya kirusi hicho cha HPV kikiingia mwilini mwake, kinaweza kwenda kuathiri chembechembe hai za mwili zilizopo kooni. “Kirusi cha HPV kikiingia kooni kinaweza kuathiri chembechembe hai za mwili na kusababisha ‘infection’, kirusi hiki kinapoingia kwenye seli huingiza vinasaba vyake, ile seli ya mwili inageuka, inakuwa na kinasaba cha kirusi hiki. “Hapo kirusi kinakuwa na uwezo wa kuanza kubadilisha ile seli na hivyo kuwa saratani, tunajua tabia ya saratani inapoingia mwilini huwa inabadilisha tabia ya seli. “Kitaalamu tunajua wazi seli za mwili huwa zinakua na kugawanyika taratibu, lakini saratani inapoingia mwilini seli za mwili huathirika na kuanza kukua kwa haraka na kugawanyika bila mpangilio. “Kwa sababu kile kirusi kinabadilisha kabisa ukuaji wa seli ndiyo maana unakuta mtu ameota nyama kubwa shingoni, yale ni matokeo ya kukua bila kudhibitiwa kwa zile seli za mwili,” alisema. Aliongeza: “Hata hivyo, uvimbe wa saratani unapoota mara nyingi huwa unaweza usiwe na maumivu ya aina yoyote ile, lakini unakua unaongezeka kwa kasi kuliko kawaida. Kijana anena Mariam Isaya (si jina lake halisi), Mkazi wa Bunju, alisema hupendelea zaidi kushiriki ngono na mpenzi wake kwa njia ya mdomo. “Huwa napata hisia zaidi nikifanya hivyo, napenda mpenzi wangu anavyonieleza jinsi anavyojisikia pindi ninapomfanyia kitendo hicho,” alisema. Alisema mpenzi wake pia huwa anashiriki naye ngono kwa njia ya mdomo na kwamba, kila wanapokutana lazima wafanye kitendo hicho. “Sina hakika na wala sijui kwamba kitendo hicho kinaweza kutusababishia kupata saratani, tumeanza kufanya hivyo kwa muda mrefu sasa na wala sifikirii na sidhani kama mpenzi wangu anafikiria kuacha, kuna raha ya kipekee,” alisema. Imegawanyika Dk. Mfuko alisema saratani ya koo imegawanyika katika sehemu mbili, ipo inayotokea katika koo la chakula na nyingine katika koo la hewa. Alisema koo la chakula lipo katika sehemu ya juu na mwendelezo wake huishia kwenye tumbo la chakula na kwa upande wa koo la hewa lenyewe huunganika hadi kwenye mapafu. “Mtu akifanya ngono kwa njia ya mdomo anaweza pia kupata saratani kwenye kinywa, sehemu ya nyuma ya ulimi, sehemu ya juu au eneo lolote hadi kwenye koo,” alibainisha. Aliongeza: “Hizi saratani za koo la chakula nazo zimegawanyika katika sehemu kuu tatu, ipo ambayo inahusisha zile zinazogusa misuli ambako ‘vocal cord’ (sauti) ndiko huwa zinatoka. “Ipo ambayo hutokea katika eneo la chini ya zile ‘vocal cord’ na nyingine hutokea eneo la juu, zote zinaweza kuwa na dalili zinazoshabihiana,” alibainisha. Utafiti wa Ocean Road Daktari huyo alisema mwaka 2008 hadi 2011 Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), ilifanya utafiti uliohusisha wagonjwa kati ya 87 hadi 90 wa saratani ya koo ambao walilazwa kwa matibabu katika kipindi hicho. Alisema matokeo ya utafiti huo yanaeleza karibu asilimia 90 ya wagonjwa waliokuwa wamepata saratani hiyo, walikuwa wanaume, wanawake walikuwa asilimia 10 tu. “ORCI walifanya utafiti huo kuangalia matokeo ya tiba, aina ya saratani na sehemu gani ya koo ilikuwa imeathirika kwa wagonjwa hao, waliangalia visababishi vitatu, walihoji iwapo walikuwa ni wavutaji sigara, watumiaji wa pombe au vyote viwili kwa pamoja. “Matokeo yao yanaonesha karibu asilimia 70 walionekana walikuwa wanatumia pombe na sigara, asilimia 12.5 walikuwa watumiaji wa sigara pekee na asilimia 18 walikuwa watumiaji wa pombe, katika utafiti huo hawakuhoji kabisa kuhusu ngono kwa njia ya mdomo,” alisema. Tafiti ya Marekani Dk. Mfuko alisema, nchini Marekani waliwahi kufanya utafiti na kugundua kwamba asilimia 35 ya wagonjwa wenye saratani ya koo nchini humo, wana ‘infection’ ya kirusi hiki cha HPV. “Kule ngono kwa njia hii ni jambo la kawaida, maana yake ni kwamba kati ya watu 100 wenye saratani ya koo watu 35 wana maambukizi ya kirusi hiki cha HPV,” alifafanua. Aliongeza: “Inaonesha kwamba ingawa inawezekana si kirusi hiki kiliwasababishia moja kwa moja kupata saratani, lakini kwa utafiti wa Marekani inaonesha watu wanaokunywa pombe wapo kwenye hatari zaidi ya kupata saratani hiyo kuliko wasiotumia. Dalili Bingwa huyo wa Mloganzila alisema, miongoni mwa dalili za awali kwamba mtu anakabiliwa na saratani hiyo, ni kupata sauti inayokwaruza, maumivu wakati wa kumeza chakula, shida ya kupumua au maumivu ya koo. “Mtu akipata shida ya kupumua anakuwa anapata shida akivuta hewa ndani huwa inatoa sauti fulani kwa sababu ile sehemu inakuwa imeziba,” alisema. Aliongeza: “Ikiwa saratani ipo kwenye koo la hewa mgonjwa hupumua kwa shida, sauti haitoki vizuri au sauti inakuwa inatokea kwa ndani pindi anapovuta hewa (stridor). “Ili kumsaidia mgonjwa wa aina hii huwa inabidi tumfanyie upasuaji wa kutengeneza njia mbadala ya kupitishia hewa, kwani tukimwacha anaweza kukosa hewa na kupoteza maisha,” alisema. Alifafanua, ikiwa ni saratani imeshambulia katika koo la chakula mgonjwa hushindwa kumeza chakula vizuri au hupata maumivu makali wakati wa kumeza. Hatari zaidi Alisema saratani inayohusisha koo la chakula ni hatari zaidi kwani sehemu hiyo ni pana, hivyo dalili huchelewa kujionesha na huanza kujitokeza wakati tayari ikiwa imeshasambaa sehemu kubwa kuliko saratani ya koo la hewa. “Mara nyingi saratani ya koo la hewa hugundulika mapema kwa sababu inapoanza tu mara nyingi sauti huwa inashindwa kupita, hivyo mtu anapokuja hospitalini anagundulika mapema na kupatiwa matibabu mapema, anapona. “Lakini kwa upande wa koo la chakula  kwa sababu dalili huchelewa kujitokeza, wengi huja hospitalini wakati tayari inakuwa imeshaanza kusambaa na ikiwa katika hatua za juu (tatu na nne) ambazo kwa kawaida huwa ngumu kutibika,” alisema. Aliongeza: “Saratani ya koo la chakula ikisambaa mno huweza pia kuathiri koo la hewa, wakati mwingine pia huweza kusababisha tezi zilizopo kooni nazo kuvimba. Uchunguzi Bingwa huyo alisema huwa wanalazimika kuchukua sampuli ya kinyama kutoka kwa mgonjwa na kwenda kukichunguza maabara ambako huwa na uwezo wa kujua ni aina gani ya saratani (koo la chakula au la hewa) na imefikia hatua gani. “Tunashirikiana kwa ukaribu na wataalamu wenzetu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI),” alibainisha. Wanaume “Kundi la wanaume ndilo lililopo kwenye hatari zaidi kupata saratani hii ikilinganishwa na wanawake kwa sababu kuu mbili, kundi hili ndilo linawatumiaji wengi wa pombe na sigara. “Hata idadi ya wanaokuja kliniki kwa matibabu tunaona wengi ni wanaume watu wazima kuanzia umri wa miaka 50 na kuendelea,” alibainisha. Alisema japo katika utafiti ule wa ORCI hawakuhusisha ngono kwa njia ya mdomo, waliangazia zaidi matumizi ya pombe na sigara, hivi sasa kuna utafiti ambao tunafanya. “Tunapochukua historia zao huwa tunawauliza iwapo wamewahi kushiriki ngono kwa njia ya mdomo, bado utafiti huo unaendelea utakapokamilika tutatoa matokeo yake,” alibainisha. Itaendelea Kesho..
0
WAWAKILISHI pekee wa Afrika Mashariki katika Ligi ya Mabingwa wa Afrika, Simba SC wamewatanguliza mashushushu nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ili kuwachunguza wapinzani wao AS Vita Club watakayokutana nao Jumamosi katika mchezo wa Kundi D.Simba inaongoza katika kundi lake, inatarajia kuondoka kesho Alhamisi kwenda Kongo tayari kucheza dhidi ya AS Vita iliyopo katika nafasi ya tatu ya msimamo wa kundi hilo.Katika mchezo wa kwanza dhidi ya klabu ya Algeria ya JS Saoura, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi jioni huku AS Vita ikifungwa 2-0 katika mchezo uliofuata dhidi ya Al Alhly ya Misri huko Alexandria.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana kuhusu mikakati yao kuelekea kwenye mchezo ujao Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Crescentius Magori alisema mipango ya maandalizi inaenda vizuri ingawa hawataki kuweka wazi mipango yao kutokana na Wakongo wengi kuishi nchini.Alisema wanaofia mipango na mikakati yao kufichuliwa, lakini alisisitiza kuwa tayari Simba imetuma watu wake `wapelezi’ kuifuatilia AS Vita na kuiandalia Simba sehemu ya kufikia na mambo mengine.“Hadi sasa tumetuma watu kuanza kufanya maandalizi ya awali kuelekea kwenye mchezo wetu na wapinzani wetu ili kuhakikisha mipango yetu ya kuvuna ushindi inaenda sawa, tunajua timu za Kongo zinajua fitina kwenye soka na ndio maana hatuwki mipango yetu yote hadharani, “amesema Magori.Amesema idadi ya kikosi kinachoondoka kuelekea kwenye mchezo huo kitawekwa wazi na kocha wa kikosi hicho Patrick Aussems muda wowote baada ya kufanya mazoezi ya jana ya kujiweka fiti kwa mchezo .Hadi sasa gharama za kusafiri mashabiki kwenda kuishangilia timu hiyo kwenye mchezo huo imeshawekwa wazi tiketi ya ndege kwenda na kurudi kwa Kenya Airways kwa Alhamisi ni dola za Marekani 760 sawa na Sh. 1,748,563 kwa siku ya Ijumaa ni dola 850 sawa na Sh. 1,955,757 wakatoi malazi ni dola 70 sawa na Sh. 161,074 wakati viza ni dola 50, sawa Sh 115,052.
4
JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limepoteza askari wake watatu waliokuwa wakishiriki kwenye ulinzi wa amani nje ya nchi. Kwa mujibu wa taarifa ya JWTZ iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, askari hao waliokufa ni Koplo Mohamed Mussa, Koplo Erick John na Praiveti Musa Machibya.Taarifa hiyo ya jeshi ilifafanua kuwa askari hao walipoteza maisha katika tarehe tofauti nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Afrika ya Kati (CAR). “Mashujaa wetu waliuawa wakiwa kwenye ulinzi wa amani baada ya kushambuliwa na vikundi vinavyosadikiwa kuwa ni vya waasi,” ilieleza taarifa hiyo ya jeshi.JWTZ ilisema kuwa miili ya mashujaa hao watatu iliwasili na kupokewa juzi kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam. Taarifa hiyo ilisema kuwa baada ya kupokewa, miili hiyo imehifadhiwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.Ilielezwa kuwa heshima za mwisho kwa mashujaa hao zitatolewa leo 3) katika sehemu ya kuagia Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo kuanzia saa 2.30 asubuhi. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linatoa mwito kwa vyombo vya habari na wananchi kuungana nao katika kuwaaga mashujaa hao.
3
VYAMA viwili vyenye ushindani wa karibu, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana vilizindua kampeni za uchaguzi wa marudio kwa vijembe katika Jimbo la Kinondoni, Dar es Salaam. CCM ambayo ilizindua kampeni zake katika viwanja vya Biafra Kinondoni na Chadema viwanja vya Ali Mapilau, karibu na Hospitali ya Mwananyamala, vimenyoosheana vidole, kila kimoja kikimwambia mwenzake hafai kuongoza jimbo hilo. Wakati CCM ikidai Chadema imekosa sera kwa sababu imekwishatekeleza karibu kila jambo, chama hicho cha upinzani nacho kimemshutumu mshindani wake huyo kuwa hakijaweza kushughulikia matatizo ya wananchi na badala yake kimesababisha hasara ya kurudia uchaguzi unaotumia fedha ambazo zingetumika kutatua kero nyingi zilizopo kama ajira, huduma za afya nk. HOJA ZA CCM Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, ambaye aliongoza mamia ya wafuasi wa CCM katika uzinduzi wa kampeni hizo, akiwa ameambatana na kada mkongwe, Stephen Wassira na viongozi wengine wa chama hicho, alisema uchaguzi huo umebeba uzito sawa na uchaguzi mkubwa. Mwigulu ambaye alikuwa akimnadi mgombea ubunge wa chama chake, Maulid Mtulia, alisema akiangalia tathimini ya hali ya kisiasa, sera na ajenda za kitaifa zote zinatekelezwa na Ilani ya CCM. Kwa muktadha huo, alisema haina haja ya kumpa kura mpinzani kwa sababu wananchi wana mkataba na CCM hadi mwaka 2020. Alisema kumpa kura mpinzani katika uchaguzi huo mdogo ni sawa na kujicheleweshea maendeleo na kumtaka kila mmoja kuwa meneja wa kampeni ili kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo. “Kama una safari na ukagundua gari ulilopanda ni bovu unashuka na kuhamia gari ambalo ni zima, sasa kule gari lenyewe hata dereva hajulikani, sasa unakaa unasubiri nini, yani hata kupe akushinde akili? “Sisi wafugaji tunajua ukiwa na ng’ombe ukamchinja, kupe wote wanaondoka haraka katika ile ngozi na kwenda kwenye ng’ombe mzima, wale watakaobaki ndio watakaukia kwenye ngozi hiyo,” alisema Mwigulu. Aliongeza kwamba anaamini kuwa kama vyama vya upinzani vingekuwa vinatekeleza wajibu wake ipasavyo, watu wasingekuwa wanavihama. Mwigulu pia alitumia fursa hiyo kutetea kile kinachotajwa kuwa hali ngumu ya kimaisha, akisema kuwa hatua zinazochukuliwa na Rais Dk. John Magufuli ni sahihi kwa sababu msingi wa uchumi siku zote ni kuwekeza fedha ili kupata fedha. “Hizi lawama za kusema eti kuna mzunguko mdogo wa fedha nchini hazina mashiko kwa sababu huwezi ukajenga reli, ukanunua ndege, kujenga mitambo ya kufua umeme, ukapanua bandari, ukatoa elimu bure halafu fedha ikawa vilevile. “Ukiishajenga reli, ukapanua bandari na ukanunua ndege sio kwamba kila mwaka utakuwa unafanya hivyo, kwa sababu kama ujenzi ukikamilika na ukianza kuzalisha fedha, unakuwa na wigo mpana wa kupandisha mishahara, unatoa ruzuku kwa wakulima, kwahiyo fedha uliyoiwekeza ukianza kuivuna ndiyo utakuwa unaitumia kwa kujidai,” alisema. Alisifia miradi inayofanywa na Rais Magufuli akisema itaishi hadi kizazi cha wajukuu zetu na hivyo kushangaa wapinzani wanapowazuia wanachama wao kuipongeza. Naye Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Wassira, alisema wapinzani wamekuwa hawana sera madhubuti na badala yake wamekuwa wakitumia uongo kujiaminisha kwa wananchi. “Wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015 walijitangaza sana mabadiliko, watu walikwenda pale Jangwani kwenye kampeni zao kwa hamasa ya hali ya juu wakisubiri mgombea wao anasema nini, cha ajabu aliposimama aliongea kwa dakika tatu tu na hotuba yake fupi kuliko sala ya ‘Baba yetu uliye mbinguni’. “Yaani alisimama na kusema elimu, elimu, elimu halafu mengine mkasome kwenye Website, sasa hawa machinga wa Kinondoni ndio wana Website? Huyo ndio alikuwa mgombea wa Chadema, alikuwa hajui ilani yao na hakuwa na cha kusema chochote,” alisema. Alisema uongo wa mabadiliko uliathiri sana Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Songwe na Mara kwa sababu wananchi walichagua mabadiliko bila kufafanuliwa ni mabadiliko ya aina ipi. “Tulifanya makosa, katika Mkoa wa Dar es Salaam mkachagua wabunge sita kati ya 10, yaani CCM ikapata wabunge wanne na wao wakapata wabunge sita,” alisema Wassira. Kwa upande wake, mgombea ubunge wa jimbo hilo, Mtulia, kwa mara nyingine tena alisema mgogoro ndani ya CUF ndio uliochangia kuhama. Alisema kwamba ilimuwia vigumu kuishi ndani ya chama hicho kwa sababu akimsikiliza katibu, mwenyekiti ananuna vivyo hivyo kwa mwenyekiti. “Nimeona jahazi linaelekea kuzama, mbele nikaona chombo cha CCM nami nimechupa nijiokoe. Jamani si mnakumbuka wenzangu wabunge 10 wa viti maalumu walichofanyiwa, sasa mlisubiri na mimi nifukuzwe? “Nilichupa kwa kujinusuru, leo nipo salama  nasimama kwenu Kinondoni, naomba tena kugombea ubunge sasa wao wananongwa ya nini, kwani huu ndio usaliti?” alisema. Aliongeza kwamba amejiunga CCM kwa sababu anampenda sana Rais Dk. John Magufuli na sifa zake zinapendwa na kila Mtanzania. Alisema amejiunga na CCM ili kuwatumikia vyema wananchi kwa sababu kuwa ndani ya chama hicho ni kujenga daraja la kuwaletea maendeleo wananchi. “Ndani ya ubunge wangu kwa miaka miwili namba ya rais sikuwanayo, lakini kwa sasa kama mgombea namba ninayo hapa, sasa wana-Kinondoni mnataka nini? Kama mnataka maendeleo sasa nakuja nayo,” alisema. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), Gaudencia Kabaka, alisema anampenda Mtulia kwa kuwa kaonyesha ushupavu kwa dhamira ya kuwatumikia wananchi wa Kinondoni kwa uhakika. Alisema Mtulia kwa sasa yupo kwenye chombo salama cha kuwaongoza wana-Kinondoni, hivyo ni wajibu wa wananchi kuhakikisha wanampigia kura za kutosha ili aibuke mshindi kwenye uchaguzi huo mdogo. “Nakumbuka pale Chang’ombe kwenye sherehe ya kupongezwa baada ya kushinda uwenyekiti wa UWT, kijana huyu Mtulia nilitambulishwa kwa mara ya kwanza, nami nilimpenda kwa uthubutu wake, kwa msingi huo sote tuhamasishane kuhakikisha tunampigia kura nyingi ili awe mbunge wetu,” alisema Kabaka. Naye aliyekuwa mgombea ubunge wa Ilala kupitia Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Muslim Hassanali, ambaye kwa sasa amejiunga CCM, alisema chama chake hicho cha zamani hakina sera ya kuwasaidia Watanzania. Alisema kwa kutambua hilo, aliona umuhimu wa kumuunga mkono Rais Magufuli kwa sababu anayoyatekeleza ndiyo matakwa yaliyokuwa yanahitajiwa na wananchi kwa muda mrefu. “Nimekuwa Chadema kwa miaka 15, nakifahamu chama hicho ndani na nje, bila saini ya Katibu Mkuu hupati posho na nimeona mengi mle, kusema ukweli hawana sera yoyote ya kuja kuwasaidia wananchi.” alisema. Alielezwa kusikitishwa na watu wanaobeza na kuwatukana viongozi, hasa kupitia kwenye mitandao ya kijamii. Katika hilo, Hassanali alimwomba Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu, kutumia kikosi cha askari wasio na mipaka (Interpol) kumkamata Mange Kimambi ambaye alidai amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kukashifu viongozi wa nchi. Kwa upande wake, Mbunge wa zamani wa Kinondoni, Idd Azzan (CCM), alisema anashukuru Mungu kutokea uchaguzi huo wa marudio ndani ya jimbo hilo, kwa sababu utawasaidia wakazi wa Kinondoni kusahihisha makosa waliyoyafanya katika uchaguzi wa mwaka 2015. Awali Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Simon Mwakifamba, alisema chama hicho kitashinda kwa goli la tikitaka huku wakiwa wamevaa msuli. HOJA ZA CHADEMA Kwa upande wake, Chadema licha ya uzinduzi wake kupambwa na msafara na umati wa wafuasi wake, pia ulikuwa na viongozi wengi wa kitaifa, wakiwamo wabunge. Waziri Mkuu wa zamani ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Edward Lowassa, aliyeongoza uzinduzi wa kampeni hizo, aliwaasa wananchi kuhifadhi demokrasia. Akimnadi mgombea wa Chadema, Salum Mwalimu, aliwataka wananchi wa Kinondoni kushughulika kutafuta kura kwani CCM haitabiriki. “Msipohifadhi demokrasia mwafa, huyu Mtulia msimsemeseme, wa nini? Shughulikieni kutafuta kura, CCM hawatabiriki,” alisema Lowassa. Lowassa ambaye aliongoza kwa kushangiliwa katika kampeni hizo, alisema alishiriki katika uchaguzi mdogo wa kata 43 na kushuhudia umati mkubwa uliojitokeza katika kampeni hizo, lakini alishangaa kuambiwa kuwa kura hazikutosha. “Salum ni kijana safi, ana uwezo wa kufanya kazi. Naomba mlinde kura, wenzetu wanatupatia kwenye kulinda. Heshima ya Chadema ni kubwa, wenzetu iko chini,” alisema Lowassa. Pamoja na hilo, Lowassa ambaye alianza kwa kuwaongoza vijana kuimba wimbo wa ‘Vijana msilale bado mapambano’, alisema alifurahi kuwaona na kwamba anawakumbuka, hivyo mbali na kura za urais mwaka 2015 kutotosha, bado ana imani iko siku zitapatikana. Mbali na Lowassa, mwingine aliyepanda jukwaani kumwombea kura Mwalimu, ni Waziri Mkuu mstaafu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye. Sumaye ambaye kama ilivyo kwa Lowassa, wote walihama CCM, alisema kazi ya mbunge ni kutetea wananchi na si kumtetea rais. “Mtulia anasema amependezwa na rais kwa kazi anazozifanya, basi akateuliwe na rais. Wewe kama umehama basi ulikuwa huelewi kazi ya mbunge, diwani, hivyo Mtulia na genge lake waache kutukana Watanzania na kudharau fedha zetu,” alisema Sumaye. Alisema fedha za kurudia uchaguzi huo zingeweza kwenda kuleta maendeleo katika sekta ya afya na elimu. Sumaye alisema CCM imewadharau wananchi kwa kumrudisha Mtulia kugombea katika jimbo lile lile alilojiuzulu. “Demokrasia ya vyama vingi ni wananchi wanapewa dhamana kuchagua na tunapokosa, tunakuwa na mvutano unaoelekeza utawala wa imla. Katiba inaruhusu maoni, lakini leo ukitoa maoni unaambiwa mchochezi,” alisema Sumaye. Alisema vikao vya Bunge wakati wa utawala wa awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais mstaafu  Benjamin Mkapa na ile ya awamu ya nne iliyoongozwa na Jakaya Kikwete vilionekana tofauti na wakati huu. Sumaye alisema mfumo wa vyama vingi hivi sasa uko zaidi katika maneno kuliko vitendo. “Tunakuwa na mfumo wa vyama vingi kwa maneno, lakini kwa vitendo hakuna, nchi itazama. Vyama vya upinzani vikifa tutazamisha nchi,” alisema Sumaye. Naye mgombea ubunge wa jimbo hilo, Mwalimu, aliposimama kwa takribani dakika tisa, alisema anatafuta kura za utumishi wa Kinondoni kwa miaka mitatu. Aliwaomba wana CCM na wale wa Chadema kumpigia kura ili akawawakilishe bungeni na kwenda kudai demokrasia, kusimamia haki masilahi na vilio vya wananchi. Alisema anafahamu changamoto zinazowakabili watu wa Kinondoni ikiwamo ajira, huduma za afya nk. Mwalimu alitumia nafasi hiyo kulikumbusha Jeshi la Polisi jinsi alivyotumia kalamu yake kama mwanahabari kulitetea na hivyo kuliomba lisimwangushe. “Nilitumia kalamu yangu kutetea Jeshi la Polisi kwa miaka tisa kupitia kituo cha Televisheni cha Chanel ten, hivyo polisi wa Kinondoni hawatapata shida,” alisema Mwalimu. Akizungumzia kuhusu soko la Tandale, Mwalimu alisema zilitengwa shilingi milioni 100, lakini mradi huo ulishindwa kukamilika kwani zinatakiwa milioni 54 nyingine hivyo aliomba kura ili akazitafute. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, ambaye pia alishangiliwa sana na wananchi wakati akipanda jukwaani, alisema watu wa Dar es Salaam wanaongea zaidi kuliko vitendo. “Ninaongea haya wakati Lissu (Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu) akiwa nchini Ubelgiji akiuguza majeraha yake, ninaongea haya wakati Sugu (Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi) akiwa mahabusu, ninaongea wakati robo ya wabunge wetu tuna kesi. Watu wa Dar mnaongea sana kuliko vitendo,” alisema Lema. Lema alisema moja ya sababu za kutoipigia kura CCM ni wabunge kushindwa kuzungumza pamoja na hali ya maisha. Alimshangaa Mtulia ambaye alikuwa mbunge na baadaye kujiuzulu kurudi tena kuomba ridhaa ya wananchi kumchagua kwenda kuwa mwakilishi wao katika Bunge lile lile. “Wanasema ‘tutaiba kura tuna dola’, wala msiogope, tunakokwenda watakuwa walinzi wazuri. Kata 43 waliiba na kupiga watu, safari hii hatukubali kwani kinga ya taifa hili ni upinzani imara,” alisema Lema. Alisema hadi wamekubali kurejea kwenye uchaguzi huu baada ya kususia uchaguzi mdogo uliopita, ni kwamba wamejipanga na hawakubali kuibiwa majimbo ya Kinondoni na Siha. Alisema vijana wasiwe waoga kwani ni dhambi kubwa, lakini pia wasifanye fujo bali waweke heshima (ushindi) siku ya uchaguzi. Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea ambaye pia ni Meneja wa Kampeni wa Mwalimu, alisema ana rekodi ya kumwangusha aliyewahi kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, marehemu Didas Masaburi kwa kura 27,000. Alisema wakati Mtulia alipochaguliwa jimboni hapo, alikodi pikipiki 300 za makamanda kwa fedha zake ili kukamilisha shughuli yake ya kuelekea kuapishwa. Kubenea alitumia fursa hiyo kueleza harufu ya ufisadi akisema wakiwa katika majukumu yao katika Halmashauri ya Jiji, walikuta majoho yakifuliwa kwa Sh bilioni 4 na laki nane, hivyo waligoma kuyafua na kuyavaa mwaka mzima. Alisema pamoja na wote kupatiwa ofisi, lakini Mtulia alipanga katika hoteli moja hapa jijini huku pia akichukua mkopo wa Sh milioni 500 benki, mkopo wa gari na fedha zake bungeni, hivyo wasimchague kumwezesha kupata tena fursa ya kukopa. Tambwe Hiza, yeye alisema aliwahi kutoroka kwenye kampeni za urais za mwaka 2015 akiwa na mtu aliyemtaja kwa jina la Mbonde ambaye kwa sasa ni marehemu ili kwenda kumnadi Mtulia. Alisema kutokana na usaliti alioufanya Mtulia, juzi alimshtaki kwa Mbonde. Tambwe ambaye alipata kuwa mfuasi wa CUF baadae CCM kabla ya kuhamia Chadema mwaka 2015, aliitaja CUF inayoongozwa Profesa Ibrahim Lipumba kama ‘Mungiki’ na kusema hawahangaiki nayo na kwamba ile ya Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad haijasimamisha mgombea. “Niliondoka CCM ili nisifie huko maana umri unaenda na dhambi ndio zinazidi. Cuf Mungiki wanatukana mitandaoni, Salum kasoma hapa tangu darasa la kwanza na anaishi hapa. Ni wa hapa, Dk. Mwinyi aliwahi kugombea bara na kisha Zanzibar,” alisema Tambwe. Akizungumza katika kampeni hizo, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema usaliti alioufanya Mtulia utakitafuna kizazi chake chote. Mbunge wa zamani wa Nyamagana, Ezekia Wenje, alihoji mwanamume anahongwaje? Naye Makamu Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick ole Sosopi, ambaye naye anaongoza timu ya kampeni, alisema vijana wamejiandaa kwa gharama yoyote kuwa jimbo hilo halitapotea huku akilinyooshea kidole Jeshi la Polisi. Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko, alisema Februari 17 iwe mwanzo na mwisho wa biashara ya kuuza watu na wananchi kuuza utu wao. Huku akilinyooshea kidole Jeshi la Polisi, alisema Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, akiwa Mkuu wa Polisi Tarime, alishuhudia kuapishwa kwa Matiko, hivyo alisema anatarajia kuona haki pia ikitendeka Kinondoni. “Polisi waache huu mchezo uwe kati ya CCM na Chadema,” alisema Matiko. Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo, alimfananisha Mtulia na bagia kuwa ilikuwa ni bidhaa iliyokuwa sokoni. Meya wa Ubungo, Boniface Jacob, alisema Kinondoni anayoijua haiwezi kuacha kufanya mabadiliko na kwamba hawawezi kuruhusu kupigwa bao. Naye Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Ilala, Dk. Milton Mahanga, alisema CCM wanamtambua kama jasusi, hivyo wamchague Mwalimu ili kukata hila. Mbunge wa Mikumi ambaye pia ni mwanamuziki wa Hip Hop Tanzania, Joseph Haule, maarufu Prof Jay, akishangliwa mara kwa mara kutokana na kusherehesha kwa kuimba baadhi ya nyimbo zake, alisema Mtulia akipita Kinondoni demokrasia itakuwa imedhalilishwa. MAANDAMANO Ufunguzi wa kampeni hizo ulipambwa na maandamano makubwa yaliyojumuisha pikipiki na magari kutoka Ofisi za Chadema Kanda ya Pwani zilizopo Magomeni hadi uwanjani hapo. Msafara wa magari hayo ulijumuisha yale ya waliowahi kuwa mawaziri wakuu, Lowassa na Sumaye.
3
BARAZA la Uuguzi na Ukunga Tanzania limemsimamisha Martin Chama kutoa huduma za uuguzi na ukunga kwa muda wa mwaka mmoja kwa tuhuma za kufi ka kazini akiwa amelewa na kutaka kuhatarisha usalama wa wagonjwa na ndugu zao kwa kushindwa kutoa huduma kwa umakini na weledi.Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga, Agnes Mtawa alisema hayo katika taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari jana Dar es Salaam.Mtawa amesema kikao cha baraza hilo cha 196 kilimsimamisha kazi muuguzi huyo Chama kuanzia Februari 7, mwaka huu kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa makosa mawili kati ya manne yaliyowasilishwa katika baraza hilo Septemba, mwaka jana.Amesema awali Ofisi ya Msajili wa Baraza hilo lilipokea tuhuma kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mount Meru Arusha kupitia kwa Muuguzi Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Msimamizi wa Maadili wa Mkoa wa Arusha kwa mujibu wa Sheria N0 1 ya Mwaka 2010.“Kwa mujibu wa taarifa hiyo muuguzi huyo alifika kazini Septemba 26, mwaka jana zamu ya usiku majira ya saa tatu usiku akiwa amelewa na alianza kuwasumbua ndugu waliokuwa wakiwaangalia wagonjwa wao kutaka kuendelea kutoa huduma kwa wagonjwa ili hali akiwa amelewa sana hali ambayo ingehatarisha maisha ya wagonjwa kwa kuwa hakuwa na umakini.“Tuhuma hizi ziliwasilishwa na walalamikaji wawili waliokuwa wakiuguza wagonjwa wao,” amesema.Alisema baada ya hapo Ofisi ya Msajili ilituma ofisa kutoka Baraza la Uuguzi na Ukunga ambaye aliungana na timu ya mkoani Arusha ikiongozwa na Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, timu ambayo ilifanya uchunguzi wa awali na kubaini upungufu uliofanywa na muuguzi huyo kinyume na Maadili ya Uuguzi na Ukunga.“Taarifa hiyo ilipelekwa katika kikao cha dharura cha Bodi cha 195 ambacho pamoja na mambo mengine kilijadili taarifa hii na kuamua shauri hili lisikilizwe katika kikao cha Bodi cha 196 ambayo itahusisha mtuhumiwa na mashahidi ambao ni walalamikaji na watumishi waliokuwepo siku ya tukio,” amesema.Aliongeza kuwa shauri hilo lilisikilizwa Februari 7, mwaka huu ambapo ushahidi uliotolewa umemtia hatiani mlalamikiwa kwa kulewa na kushindwa kutoa huduma kwa wagonjwa kwa weledi na kutaka kuhatarisha maisha ya wagonjwa na ndugu zao.Baraza la Uuguzi na Ukunga ni Mamlaka iliyoanzishwa kisheria na kufanya kazi chini ya Sheria inayoitwa The Nursing and Midwifery Act, of 2010.Baraza lilianzishwa kwa ajili ya kulinda umma kutokana na huduma zinazotolewa na wauguzi na wakunga nchini na linafanya kazi kwa kusimamia ubora katika mafunzo na kuhakikisha huduma zinazotolewa zinazingatia viwango vilivyowekwa.
3
KOCHA mpya wa Tottenham, Jose Mourinho anasema kuwa katika klabu yake mpya ya Spurs kamwe hatafanya makosa aliyoyafanya huko nyuma katika majukumu yake ya ukocha.Mreno huyo amechukua nafasi ya Mauricio Pochettin Jumatano, akihitimisha miezi 11 ya kutofanya kazi ya ukocha tangu alipotimuliwa Manchester United. Mourinho alijielezea kama mtu mnyenyekevu katika mkutano wake wa kwanza kama kocha wa Spurs, akisema alitumia muda wake nje ya soka akielezea taaluma yake.“Niligundua kuwa nilifanya makosa,”alisema.“Sitafanya tena makosa yale yale. Sasa nitafanya makosa mapya, lakini si yale yale.” Mourinho, ambaye hata hivyo, hakuweka bayana makosa anayoyazungumzia, aliongeza: “Mimi ni mnyenyekevu katika kazi yangu, na sio kwa mwaka jana ila kwa kila kitu, kuhusu mabadiliko, matatizo na ufumbuzi. Simlaumu mtu yeyote.“Ni jambo kubwa. Nilikwenda mbali zaidi…, “alisema kocha huyo mwenye maneno mengi.Mourinho kipindi chake akiwa Manchester United kilimalizika Desemba mwaka jana baada ya timu hiyo kuwa pointi tisa nyuma ya vinara wa Ligi Kuu, Liverpool. Pia aliripoti kufeli katika usajili wake wa Paul Pogba ambao uligharimu kiasi cha pauni milioni 89, ambao ulikosolewa na mashabiki. Kocha huyo wa zamani wa Porto, Chelsea na Real Madrid aliondoka Old Trafford akiendeleza tabia yake ya kutomaliza misimu minne mfululizo katika klabu moja.“Nisiposhinda kamwe siwezi kuwa na furaha na hilo siwezi kulibadili,” aliongeza Mourinho.“Hiyo ndio alama yangu. “Natumaini naweza kuwashawishi wachezaji wangu, kwa sababu ikiwa unafurahia kushindwa mechi ya soka ni vigumu sana kuwa mshindi. “Wakati fulani unatakiwa kufanya kazi na watu, ambao huwapendi na kufanya kazi vizuri. Huo ndio utaratibu wetu na sifikiri kama naweza kuubadili.”WACHEZAJI WAPYAMourinho alitumia kiasi cha pauni milioni 400 kwa kununua wachezaji wapya 11 wakati wa miaka yake miwili pale Manchester United, lakini anaamini tayari ana wachezaji wazuri hapo Spurs.“Zawadi kubwa niliyokuwa nayo mimi, sihitaji wachezaji wapya,”aliongeza.“Kwa kweli nina furaha na hawa nilionao hapa. “Kikubwa nahitaji muda zaidi wa kuwa na wachezaji hawa. Nawajua kutokana na kucheza dhidi yao, lakini huwezi kuwajua vizuri sana.”Kocha huyo mwenye umri wa miaka 56 ameanza kuifundisha timu hiyo ya Spurs ambayo iko katika nafasi ya 14 katika msimamo wa Ligi Kuu ya England ikiwa imeshinda mechi tatu tu msimu mzima hadi sasa.Hata hivyo, Mourinho, ambaye ameshinda mataji katika kila klabu aliyoifundisha, ana uhakika bahati ya klabu hiyo itarejea baada ya yeye kutua hapo.Alisema: “Hatuwezi kutwaa taji la Ligi Kuu msimu huu, lakini tunaweza kushinda msimu ujao…” Licha ya Tottenham kuanza vibaya msimu, kuondoka kwa Pochettino Jumanne kulitokea kama kwa mshangao kwa wengi baada ya klabu hiyo kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu uliopita na kufungwa na Livepool.
4
Zainab Iddy, Dar es Salaam BAADA ya Serikali kusimamisha  Ligi Kuu Tanzania Bara sambamba na michezo mingine yote kwa siku 30 , baadhi ya wachambuzi wa soka nchini wamesema kuwa   suala la ukata halitokwepeka  pale mashindano yatakapoendelea. Juzi Serikali kupitia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa , alitangaza kusitisha shughuli zote zinazosababisha mikusanyiko ya watu ikiwemo michezo kama njia ya kuchukua tahadhari ya kuenea kwa ugonjwa wa Corona ulioonekana kuwa janga  ulimwenguni kote. Wakizungumza na MTANZANIA jana, kwa nyakati tofauli wachambuzi hao walisema  ni jambo zuri lililofanywa na serikali lakini lazima Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lifahamu pale ligi zitakapoendelea kutakuwa na tatizo kubwa la uchumi kwa wanachama wao. “Kila mmoja nafahamu jinsi  baadhi ya timu zilivyokuwa zinaendeshwa kiugumu hadi baadhi kushindwa kutoka kituo kimoja kwenda kingine, hivyo kusimama kw aligi kutaongeza maumivu zaidi ya yale ya kwanza. “Bila shaka kuna  timu zilishapambana kutafuta fedha zitakazoweza kuwasaidia kumaliza ligi, walipozipata walilipa gharama mbalimbali hadi mwisho wa msimu  kabla ya muda kufika yametokea haya ni vigumu kurejeshewa gharama zao kama walivyotoa, “Lakini pia wamelazimika kuwapa nauli wachezaji ili warejee  katika familia zao, hivyo watata kiwa kuja kuwarejesha pia, hii ni kazi mara mbili,” alisema Ally Mayay. Kwa upande wake, Alex Kashasha alisema : “ Bajeti iliyokuwa imedundulizwa haikuwa inatosha, kwa hili lililotokea timu lazima ziingie gharama kwa sababu siku zote inapotoka ratiba huwa zinajipanga kulingana na ratiba,  kutokana na mabadiliko haya TFF ijiandae kupokea kesi nyingi za madai. “ Madhara mengine yataonekana kwa wachezaji mmoja mmoja, bila shaka viwango vyao vitashuka kwa sababu muda mwingi watakuwa katika nyumba zao na wachache watakuwa na akili ya kufanya mazoezi binafsi hili litasababisha ligi ijayo au itakapoendelea kupoteza mvuto,”alisema Kashasha.
4
Juhudi za kocha Ole Gunnar Solskjaer kuimarisha kikosi chake huenda zikagonga mwamba kwa sababu Manchester United ni klabu ambayo hutoa ofa ya chini kwa wachezaji wanaotaka kuwasajili. (Evening Standard) Solskjaer anataka kumuuza kiungo wa kati wa Man Utd Mfaransa Paul Pogba, 26, bada ya kufahamishwa kuwa ana pauni milioni 100 ya kuwasajili wachezaji wapya msimu huu. (Star) Mchezaji nyota wa kimataifa wa Brazil Neymar, 27, hana mpango wa kuchezea tena Paris St-Germain. (Sport – in Spanish) Real Madrid wameweka dau la euro milioni 130 kumnunua Neymar, kutoka PSG, mshambuliaji wa Wales Gareth Bale, 29, au mshambuliaji wa Colombia James Rodriguez, 27. (Mundo Deportivo – in Spanish) Atletico Madrid wanakaribia kukamilisha sajili wa Joao Felix wa Benfica kwa kima cha euro milioni 120 sawa na (£106.7m) hii ina maanisha Manchester United watamkosa kiungo huyo wa kimataifa wa Ureno aliye na umri wa miaka 19. (Evening Standard) Kiungo wa kati wa Atletico Madrid Mhispania Rodri, ameamua kujiunga na Man City badala ya Bayern Munich na kuhamia City kawa malipo ua £62m. (Kicker – in German) Manchester City wanapigiwa upatu kuipiku Man Utd katika usajili wa Harry Maguire, 26, kutoka Leicester kwa kima cha pauni milioni 65 baada ya kiungo huyo wa England kupita vipimo vya matibabu. (Star) Man City wanatafakari uwezekano wa kumsaini kwa mkataba wa bure Asier Riesgo wa ibar na kumfanya Mhispania huyo wa miaka 35 kuwa kipa wao wa tatu. (Manchester Evening News) Everton wameanza maungumzo na Chelsea kuhusu usajili wa Kurt Zouma kwa mkataba wa kudumu baada ya mlinzi huyo wa Ufaransa, 24, kucheza Goodison Park msimu uliopita kwa mkopo katika. (Telegraph) Tottenham wamefanya mazungumzo na ajenti wa kiungo wa kati wa Ureno Bruno Fernandes, 24, kuhusu uhamisho wake kutoka Sporting Lisbon. (Telegraph) Juventus wana matumaini ya kufukia mkataba wa kumsaini Adrien Rabiot kutoka Paris St-Germain, huku mkataba wa mchezaji huyo raia wa Ufaransa anaechezea safu ya kati ukitarajiwa kukamilika msimu huu wa joto. (Goal) Liverpool hawana mpango wa kumuuza Divock Origi msimu huu wa joto licha ya mshambuliaji huyo wa Ubelgiji mweye umri wa miaka 24 kusalia na mkataba wa mwaka mmoja. (Liverpool Echo) Tetesi Bora Alhamisi Chelsea inapania kumuajiri kocha wa Derby Frank Lampard, kama maneja wake mpya kwa kandarasi ya miaka mitatu kufikia mwisho wa wiki hii. (Standard) Inter Milan na Atletico Madrid wanataka kusajili beki wa England anaechezea klabu ya Southampton Ryan Bertrand, 29. (Mail) Juventus wanaamini wataipiku Real Madrid katika usajili wa kiungo wa kati wa Manchester United na Ufaransa Paul Pogba, 26. (Mirror) Ajenti wa Gareth Bale amepuuziliambali madai kuwa mshambuliaji huyo wa Real Madrid wa miaka 29 huenda akahamia Bayern Munich kwa mkopo. (Mirror) Arsenal wanajianda kuweka dau la kumnunua winga wa Red Bull Salzburg na Hungary Dominik Szoboszlai, 18. (Football Insider) Kipa Tom Heaton amekataa ofa ya kandarasi mpya aliyopewa na Burnley. Kipa huyo wa kimataifa wa England mwenye umri wa miaka 33 ataingia mwaka wake wa mwisho wa mkataba wake wa sasa katika uwanja waTurf Moor mwezi ujao. (Guardian  
4
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara, Simba na wawakilishi wa nchi katika Kombe la Shirikisho Afrika, Yanga leo watashuka kwenye viwanja viwili tofauti kujipima nguvu. Simba itachuana na Bandari ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa huku Yanga ikicheza na timu ya Daraja la  Kwanza ya Friends Rangers kwenye mazoezi yao ikiwa ni sehemu ya kujipima nguvu kwa maandalizi ya michezo ijayo ya ligi. Katika mchezo wa wekundu hao wa Msimbazi wameamua kutumia muda huu wa mapumziko mafupi ya ligi kuendelea kujiimarisha kuelekea katika mchezo ujao wa ligi dhidi ya Azam FC utakaochezwa Oktoba 23, mwaka huu. Lakini pia, ni mchezo muhimu sio tu kwa mwenyeji bali hata wageni Bandari wanaojiandaa na mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika. Wekundu hao waliwahi kukutana na Bandari Januari mwaka huu kwenye michuano ya SpotiPesa na kufungwa mabao 2-1. Timu zote ni nzuri Simba ikiongoza ligi nchini kwa pointi 12 katika michezo minne huku Bandari ikishika nafasi ya nane Kenya katika michezo mitano iliyocheza ikiwa na pointi nane. Leo Simba itawakosa karibu wachezaji tisa muhimu wanotumikia timu ya taifa na wawili ni majeruhi muda mrefu ambao ni Gadiel Michael, Jonas Mkude, Mohamed Hussein, Erasto Nyoni, Miraji Athumani, Clatous Chama Zambia na Meddie Kagere Rwanda huku Shomari Kapombe na John Bocco wakitajwa kuwa ni majeruhi. Kwa upande wa Yanga imepanga kucheza na Rangers kwenye mazoezi kati ya uwanja wa Polisi au Gyhm- khana katika kuwapima wachezaji waliopo baada ya baadhi ya kwenda kwenye timu ya taifa na wengine ni majeruhi. Wachezaji ambao hawapo ni Farouk Shikalo, Metacha Mnata, Kelvin Yondani, Abdulaziz Makame na Feisal Salum lakini wengi wapo na baadhi waliokuwa majeruhi kama Paulo Godfrey na Issa Bigirimana wamerejea.Yanga inajiandaa na mchezo miwili ya ligi itakayochezwa kanda ya ziwa na michezo ya Kombe la Shirikisho na inatarajiwa kukabiliana na Pyramid ya Misri katika hatua inayofuata.
4
NAIROBI, KENYA MWANASHERIA Mkuu wa Serikali ya Kenya, Profesa Githu Muigai, amemuonya Kiongozi wa Muungano wa Upinzani wa National Super Alliane (NASA), Raila Odinga kwamba anakabiliwa na adhabu ya kifo iwapo ataapishwa kuwa ‘rais wa wananchi.’ Katika hilo, Profesa Muigai aliwashutumu mawakili wa upinzani kwa kuwapotosha Wakenya kuhusu kuapishwa kwa Raila, akisema hilo ni kosa la uhaini ambalo hukumu yake ni adhabu ya kifo. “Inasikitisha kuona baadhi ya mawakili nchini, wenye hadhi ya kuitwa mawakili waandamizi, wanapotosha eti kosa la uhaini halitambuliwi katika Katiba ya sasa,” alisema Profesa Muigai akionekana kumlenga Seneta James Orengo aliyedai kuwa kosa la uhaini halitambuliwi. Pia anayekabiliwa na hatari hiyo ya kushtakiwa kwa uhaini ni aliyekuwa mgombea mwenza wa Raila wakati wa Uchaguzi Mkuu, Kalonzo Musyoka, ambaye alitarajia kuwasili juzi jioni kutoka Ujerumani, ambako amekuwa akimuuguza mkewe kwa miezi miwili sasa. Haijafahamika iwapo Musyoka ataapishwa sambamba na Raila, lakini inatarajiwa Makamu Rais huyo wa zamani ataweka wazi mipango yake siku si nyingi kuanzia jana. Profesa Muigai alisema kitendo hicho ni kinyume cha Katiba na sheria husika, na kuongeza kuwa kuna rais halali ambaye ni Uhuru Kenyatta. “Idara ya Polisi, Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) na Idara ya Mahakama zimejiandaa kupambana na mtu au kundi lolote la watu ambao watathubutu kufanya mapinduzi ya aina yoyote dhidi ya Serikali halali iliyoko mamlakani,” alisema. Profesa Muigai alisema ni wajibu wa polisi na asasi nyingine huru kuhakikisha kuwa kila Mkenya bila kujali hadhi yake kijamii na kisiasa, anatii sheria. “Asasi hizi zitatekeleza majukumu yake wakati ufaao, iwapo mtu yeyote atadiriki kuvunja sheria,” aliwaambia wanahabari juzi Jumatatu asubuhi bila kumtaja Raila moja kwa moja.
2
Na KULWA MZEE-DODOMA MBUNGE wa Mbozi, Pascal Haonga (Chadema), amemwomba Rais Dk. John Magufuli kujaza nafasi za aliyekuwa Naibu Waziri (Ofisi ya Waziri Mkuu), Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Dk. Abdallah Possi na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ili wabunge wa CCM watulie. Nafasi ya Dk. Possi iko wazi tangu Januari mwaka huu alipoteuliwa kuwa balozi, huku ya Profesa Muhongo ikiwa wazi tangu Mei 24, uteuzi wake ulipotenguliwa na Rais Magufuli kutokana na uchunguzi wa ripoti ya kwanza ya makinikia. “Namuomba Rais ajaze nafasi ya Profesa Muhongo na Possi, kwa sababu nimeona kuna baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanashindana kutafuta nafasi hizo kwa kushambulia upande huu. Kwa hiyo naomba niseme tu kwamba, afanye uteuzi huo haraka,” alisema Haonga alipopewa nafasi ya kuchangia Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2017/18 bungeni jana. Kabla ya kumaliza, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, aliyekuwa akiendesha kikao cha asubuhi, alimkatisha kwa kusema “wewe changia bajeti, acha haya mambo”. Baada ya maelezo hayo, Haonga alisema: “Mheshimiwa mwenyekiti, baada ya ushauri huo naomba sasa niendelee kuchangia bajeti iliyo mbele yetu.” PAULINE GEKUL Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul (Chadema), akichangia bajeti, alisema Serikali inatakiwa kuwa wazi ili wabunge waishauri kwani kwa kuleta vitu vya mafungu hawatapata nafasi ya kuishauri. “Kwa sasa Serikali imekusanya asilimia 70, leo mnaleta trilioni 31/- wakati makusanyo ni asilimia 70. Mgetuambia ukweli wapi mmekwama kuliko kuleta makadirio makubwa. “Serikali imepanga kuzimisha kabisa Serikali za Mitaa, vyanzo vyote mmeshindwa mnakuja kuchukua katika vyanzo vyetu huku. “Bajeti hii ya kuua Serikali za Mitaa kwa asilimia 100, kwani hadi sasa Serikali haijakusanya kodi ya majengo, ni bora mngetuachia sisi halmashauri tukakusanya. “Sasa hivi mmetuachia makusanyo ya kodi katika masoko na stendi, wakati kuna watu wanahitaji mishahara na vyanzo hakuna. “Fedha mnazokusanya mnadai mtarejesha, ni uongo hazirejeshwi, leo mnataka tuwatoze faini ya Sh 100,000, 200,000 hadi Sh 1,000 mtu akitupa taka, hata katika rambo, ilikuwa Sh 50,000 mmepandisha. “Mmepandisha faini kutoka Sh 50,000 hadi milioni, hicho ndiyo chanzo mlichotuachia, kwanza hiki chanzo hakiwahusu, ni sheria ndogo za halmashauri,” alisema. Alisema Serikali Kuu imeamua kunyonga halmashauri zote. WILLIAM NGELEJA Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), alisema anaungana na wote wanaounga mkono bajeti hiyo asilimia 100. Alisema Sengerema kuna mradi mkubwa wa maji ambao tayari umekamilika, kuna miradi kadhaa imebuniwa na kwamba bajeti hiyo imezingatia vizuri jimboni kwake. “Hatuwezi kuzungumzia viwanda bila kuwa na umeme wa uhakika, viwanda na reli inayojengwa vyote vinahitaji umeme mwingi sana. “Kuna haja ya kushirikisha sekta binafsi kushirikiana na Serikali kuwekeza katika vyanzo vya umeme,” alisema. JANET MBENE Mbunge wa Ileje, Janet Mbene (CCM), alisema tozo ya mazao ifanyiwe kazi kwa kuweka tozo moja kwa mazao yote ya biashara na chakula. Alisema pamoja na kuorodhesha kodi, TRA ianze kutoa elimu ya kulipa kodi, wafahamishwe walipakodi wanalipaje ili kupunguza usumbufu. Alisema miradi ya kimkakati imekuwa ya siku nyingi, hivyo imalizwe mikataba ya uwekezaji, ulipaji wa fidia ili miradi ya mkakati ifanye kazi.
3
BADI MCHOMOLO KILA Ufalme una mwisho wake, hakuna kitu kizuri kama kumaliza Ufalme wako huku watu wakiwa bado wanakuhitaji. Eldrick Tont, maarufu kwa jina la Tiger Woods ni nyota wa mchezo wa Gofu duniani akiwa raia wa nchini Marekani, mbali na kuwa hodari kwenye mchezo huo, lakini anatajwa kuwa mmoja kati ya wanamichezo wenye ushawishi mkubwa duniani. Huyu ni staa ambaye aliwahi kutikisa dunia katika mchezo huo pamoja na kuwa mwanamichezo ambaye anaongoza kwa kulipwa fedha nyingi miaka ya nyuma kutokana na ubora wake. Staa huyo mwenye umri wa miaka 43, alianza kuwika katika mchezo huo huku akiwa na miaka 20, ilikuwa mwaka 1996 na mwaka mmoja baadae akaweza kuwa namba moja kwa ubora duniani. Aliweza kudumu kwenye ubora huo hadi ilipofika 2010, lakini alianza kushuka kiwango baada ya kutangaza kuwa yupo kwenye mipango ya kufunga ndoa na mpenzi wake Elin Nordegren na baada ya kufunga ndoa miezi michache baadae alitangaza kuachana. Woods alitajwa kuwa mwanaume ambaye sio mwaminifu kwa mkewe, alikuwa na wasichana wengine pembeni na ndio maana ndoa yake haikudumu, kitendo hicho kilimfanya staa huyo akosolewe kwa kiasi kikubwa na kusababisha kiwango chake kushuka. Ilivyofika 2011, nyota huyo katika orodha mpya ya wachezaji bora wa Gofu alijikuta akiangukia kwenye nafasi ya 58, kitendo hicho kiliwashtua mashabiki wake wengi, lakini aliwatoa wasiwasi na kuwaambia lazima arudi katika nafasi yake walioizoea. Aliweza kupambana kwa miaka miwili na ilipofika Machi 2013 aliweza kurudi kwenye ubora wake na kushika nafasi ya kwanza, aliweza kudumu hadi Mai 2014. Kwa kuwa alikuwa anatumia nguvu nyingi katika mazoezi ili kuweza kurudisha kiwango chake, alijikuta akipatwa na maumivu ya mgongo na mkono. Majanga yalianza kumkuta mwaka 2013 baada ya kufanyiwa upasuaji wa mkono, lakini mwaka 2014 majanga yalizidi kwa kuwa alifanyiwa upasuaji wa mgongo mara nne kwa vipindi tofauti, hivyo hakuweza kuwa vizuri kwenye ushindani na kujikuta jina lake kwenye mchezo huo likipotea. Mwaka 2017, alionekana kuingia kwenye ulevi, hivyo aliwahi kukamatwa na polisi na kuwekwa ndani kutokana na kuendesha gari huku akiwa amekunywa pombe na ametumia dawa za kulevya. Hapo ndipo ndoto zake za kurudi kwenye nafasi ya kwanza au 10 bora ikaanza kugonga mwamba hasa kutokana na hali yake. Kutokana na matatizo hayo, Woods alitangaza kuwa anataka kustaafu mchezo huo kutokana na kashfa anazokumbwa nazo pamoja na hali ya afya yake. Alikaa muda mrefu bila ya kushiriki michuano mikubwa, hata hivyo mara ya mwisho kuchukua taji kubwa ilikuwa mwaka 2008, hivyo hakuna aliyeamini kama ataweza kuja kuwa bora tena kama ilivyo zamani. Mbali na kashfa zote hizo, lakini wiki iliopita staa huyo alirudi kwenye ufalme wake na kutwaa taji kubwa la mchezo huo ambalo linajulikana kwa jina la Masters, huku ikiwa ni miaka miwili tangu alipotangaza nia ya kutaka kustaafu. Haikuwa kazi rahisi kuchukua ubingwa huo, alitumia nguvu nyingi sana kufanikisha hilo, lakini hatimaye ameweza kuandika historia nyingine mpya ambayo imeshtua wengi ikiwa pamoja na Rais wa Marekani, Donald Trump. Imefikia hatua rais huyo amepanga kutaka kumpa tuzo ya heshima kutoka Ikulu hasa kwa kuthamini kile alichokifanya kwa kipindi chote cha maisha yake ya mchezo huo pamoja na kurudi kwa nguvu na kutwaa taji hilo baada ya kukumbwa na majanga mbalimbali kwa kipindi cha miaka 11. Huu ni wakati wake sasa wa kufanya maamuzi sahihi ya kuamua kustaafu mchezo huo kwa kuwa taji kubwa ambalo alikuwa analitafuta amefanikiwa, hakuna kitu kingine ambacho anakitafuta. Umri wake unaruhusu kustaafu hasa kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya mgongo. Akistaafu muda huu litakuwa jambo sahihi kwa kuwa atakuwa amelinda heshima yake kwa kustaafu huku akiwa na taji kubwa mkononi la Masters. Taji hilo limemfanya ajisafishe kwa yale mabaya aliyoyafanya kipindi cha nyuma, hivyo hatakiwi kustaafu huku akiwa kwenye kiwango cha chini au akiwa kwenye matatizo, anatakiwa kustaafu huku akiwa anazungumziwa kwa jambo kubwa alilolifanya itakuwa analinda heshima yake kwa kiasi kikubwa.
4
ZIKIWA zimepita siku tano tangu ilipoanza operesheni kali ya kukamata wanaoghushi risiti za kielektroniki (EFD) Kariakoo jijini Dar es Salaam, sasa imeanza kufanyika nchi nzima.Maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wanafanya msako mkali kubaini wanaoiibia Serikali.Hatua hii inakuja siku chache tu tangu gazeti hili lilipochapisha ripoti maalumu iliyonesha jinsi baadhi ya wafanyabiashara katika eneo la Kariakoo wanavyoiibia serikali.Aidha, kupitia operesheni hiyo, mamlaka hiyo imesema kuwa watakaokamatwa watalipa faini, kufungwa jela au mizigo yao kutaifishwa.Katika operesheni kali inayoendelea katika eneo la Kariakoo ambapo baadhi ya wafanyabiashara na wateja wao walikamatwa na risiti feki huku wengine wakikutwa wakiuza bidhaa bila kutoa risiti.Mkurugenzi wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi mamlaka hiyo, Richard Kayombo aliliambia gazeti hili kuwa mamlaka hiyo imeamua kuifanya operesheni hiyo kitaifa na iwapo yeyote atabainika, hatua kali zitachukuliwa.Alisema,"Tulianza na operesheni juzi (Jumatano) katika eneo la Kariakoo lakini sasa inahamia nchi nzima, haiwezekani watu wakakiuka sheria tukawavumilia huku serikali ikipoteza mapato."Tunaendelea kutoa elimu juu ya faida ya kulipa kodi lakini kuna wasiowaaminifu ambao wanaiba tena kwa kughushi risiti... "...wengine wanatoa risiti ambazo hazielezi thamani halisi iliyotolewa na mteja lakini pia wengine wanatumia risiti moja kusafirisha mizigo tofauti kwa nyakati tofauti," alisema Kayombo na kueleza kuwa maofisa wa mamlaka hiyo kwenye mikoa mingine ya Kodi wanaendelea na kazi hiyo.Aidha, alitoa tahadhari kuwa wanaofanya hivyo kuwa wakikamatwa watalipa fidia kubwa, kufungwa jela au hata bidhaa zao kutaifishwa.Alisema,"Tukikubaini, lazima ulipe faini au faini na kifungo. Na kama mzigo wako utakamatwa basi tutauchukulia kuwa ni mzigo usiokuwa na mwenyewe kwani risiti halisi ya TRA ndiyo utambulisho wa mzigo iwapo umenunuliwa."Katika mji wa Babati mkoani Manyara, mfanyabiashara Isaac Mushi ambaye anafanya biashara ya vifaa vya umeme alisema kuwa maofisa hao wamefika kwenye eneo lake la biashara na kuchunguza iwapo risiti za EFDs zinazotolewa zinakabidhiwa na kutumika kwa usahihi na kwamba juhudi hizo ni nzuri kwa faida ya taifa.Alisema, "Nilisoma kwenye gazeti la HabariLeo Jumatatu iliyopita, liliandika kuhusu jinsi walipa kodi wanavyoiibia Serikali. Kwa kweli kama mfanyabiashara nilisikitika kwani hao wanaofanya hivyo wanafanya kuhujumu maendeleo ya nchi."Ni kweli kila mfanyabiashara anataka faida, tena iliyo kubwa lakini tunapaswa kutambua kuwa Serikali nayo inahitaji fedha kwa ajili ya kuleta maendeleo kama barabara na umeme."Maendeleo hayo yakishaletwa, na sisi kazi inakuwa rahisi, uwezekano wa kuongeza kipato unakuwa mkubwa," alisema mfanyabiashara huyo aliyezungumza kwa njia ya simu huku akiipongeza mamlaka hiyo ya mapato kwa kile inachokifanya.Yohana Maduhu ambaye ni mfanyabiashara mwenye duka la vinywaji katika mtaa wa Uhuru jijini Mwanza alisema kuwa maofisa wa TRA hufika mitaa hiyo mara kwa mara kwa ajili ya ukaguzi, jambo ambalo linaashiria uwajibikaji.Maduhu alisema, "Awamu hii, watu wanafanya kazi, lakini hili suala la kodi niseme tu ni kwamba tunalipa. Kama wako wanaodanganya basi watakamatwa kwani serikali ina mkono mrefu na inaweza kuwabaini wote wanaofanya kinyume na utaratibu."Mmoja wa wafanyabiashara mkoani Mbeya, Aristus Nonga aliliambia gazeti hili kuwa hajashuhudia ukaguzi unaofanywa kwenye mkoa huo isipokuwa ana taarifa kuwa kuna maofisa wanaoshtukiza kwenye maduka na kwamba zoezi hilo limetiliwa mkazo baada ya kubainika kuwepo kwa wafanyabiashara Kariakoo ambao wamekithiri.
5
MWAKA 2018 unaoeleka ukingoni, umetawaliwa na mijadala mingi kuhusu sekta ya elimu nchini, hasa hoja ya ubora wa elimu, hatma ya elimu bila malipo, uhaba wa miundombinu, vifaa na walimu.Hii ni kwa kuwa elimu ndicho chombo pekee anachoweza kukitumia mwanadamu katika kumtii Mungu kwa kujua halali na haramu na akapambanua baina ya lenye kunufaisha, au lenye kudhuru jamii na ili Tanzania nayo ipige hatua kimaendeleo, elimu haina budi kutazamwa kwa macho yote. Ndiyo maana Mwaka 2018 Watanzania wanashuhudia mjadala mkali ukiendelea ndani na nje ya nchi kufuatia kauli ya Rais John Magufuli aliyoitoa wakati akihitimisha ziara ya siku tatu mkoani Pwani Juni 2017, kuhusu wanafunzi wa kike wanaopata mimba kutorudi kuendelea na masomo katika shule za Serikali.Huu ni msimamo unaooungwa mkono na taasisi nyingi za dini ambazo pia, haziruhusu watoto kupata mimba katika hali ya kawaida, katika shule zao, kisha kuendela na masomo. Hilo, limeungwa mkono na Watanzania wengi wanaotaka taifa kuwa na watu waadilifu. Mengine yaliyoteka mijadala katika sekta ya elimu nchini mwaka huu, ni kufutwa kwa matokeo ya darasa la saba, ongezeko la ufaulu kwa darasa la saba, suala la ni lugha ipi ya kufundishia na ufunguzi wa maktaba ya kisasa na Kituo cha Kichina katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Kauli na msimamo wa kiuadilifu ya Serikali ‘kutowafungulia watoto kuchezea maisha shuleni” hadi kupata ujauzito wakiwa masomoni, inaigusa hadi Benki ya Dunia (WB) inayotishia kuzuia msaada wa Dola milioni 300 kwa Tanzania hadi suala hilo litakapowekwa vizuri, lakini hatimaye ‘ikaachia.’ Pia suala la ubora wa elimu halikuachwa nyuma mwaka 2018 kufuatia serikali kutekeleza mpango wa elimu msingi bila malipo ulioanza mwaka 2016, likawaibua watu wengi wakiwemo viongozi wastaafu, wabunge n.k. Mwaka huu kunaibuka maoni tofauti kuhusu utoaji huo wa elimu, na baadhi ya watu wanadhani ongezeko la uandikishwaji wanafunzi wa shule za msingi nchini haliendani na ubora wa elimu.Machi 18, 2018 Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa anasema kuna janga katika elimu nchini na kushauri kuitishwa kwa mdahalo wa wazi utakaoshirikisha makundi yote ya jamii ili kujadili suala hilo. Anayasema hayo wakati akishiriki katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Profesa Idris Kikula. Hoja hiyo inawaibua wadau wengine wa elimu walioeleza udhaifu uliopo katika elimu nchini ikiwemo kuibua kasoro zilizopo katika baadhi ya vitabu vya shule.Kwa mfano, mhasibu wa kujitegemea nchini, Robert Chiwango anabainisha kuwa, kitabu cha Somo la Hisabati cha Kidato cha Tatu kilikuwa na makosa yaliyosababisha wanafunzi kufeli somo hilo tangu kilipoanza kutumika mwaka 2008. Hata hivyo, Naibu Waziri wa Elimu, William ole Nasha anabainisha kuwa, suala la vitabu vyenye makosa limeshajadiliwa na tayari serikali imekwishachukua hatua ya kuviondoa kwenye mzunguko.Halikadhalika, mjadala kuhusu lugha ya kufundishia unachukua nafasi kubwa mwaka 2018, licha ya kuwa ni mjadala wa muda mrefu, kwani ulianza tangu Tanzania ilipopata uhuru mwaka 1961. Mjadala huu unawagawa wasomi katika kambi mbili, moja ikitetea Lugha ya Kiingereza na wengine wakitaka Kiswahili kitumike kufundishia katika mfumo wote wa elimu. Agosti mwaka huu, Taasisi ya HakiElimu inaandaa mdahalo. Mhadhiri na mtaalamu wa Lugha ya Kiingereza, Dk Michael Kadeghe anasema haamini kuwa Kiswahili ni suluhisho la elimu bora.Mhadhiri wa Elimu kutoka Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu (DUCE), Dk Luka Mkonongwa anasema lugha si kigezo cha wanafunzi kufeli mitihani. “Lugha ni kitu kidogo, ila mifumo tunayotumia kufundishia, maarifa aliyo nayo mwalimu na mazingira aliyo nayo mwanafunzi ndivyo vinavyotakiwa. Lugha ni kitu kidogo tu. Tunasema Kiingereza ni lugha ya kigeni, siyo kweli.Tumekuwa nayo miaka 50 sasa, wataalamu wote wamefundishwa kwa Kiingereza halafu tunageuka tunasema ndiyo shida,” anabainisha. Hata hivyo, licha ya safari ndefu ya kukipigania Kiswahili, watetezi wake hawajakata tamaa. Katika wasilisho lake, Profesa Mshiriki kutoka Kitengo cha Stadi za Mawasiliano cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Martha Qorro anasema, kamati zaidi ya 20 zilizofanya utafiti zilithibitisha kuwa Kiingereza hakifai kufundishia. Anasema, nchi zinazoendelea zimerithi mfumo wa elimu kwa maslahi ya wakoloni, ndiyo maana kila nchi ya Afrika inatumia lugha ya nchi iliyoitawala.Anahimiza kila mwanajamii kujiuli kuwa, sisi ni nani na tunakwenda wapi. Akiunga mkono matumizi ya Kiswahili, Profesa Aldin Mutembei kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anawalaumu wamiliki wa shule za binafsi kuwa wanatetea Kiingereza kwa sababu za kibiashara. Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, Dk John Kallaghe yeye anasema mgawanyiko wa mawazo si tu umeathiri mfumo wa elimu nchini, bali pia umezalisha aina mbili tofauti za wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu katika mfumo mmoja.Oktoba 2018, Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) linaweka historia ya kufuta matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi (darasa la saba) mwaka 2018 kwa watahiniwa 357 na baadhi ya shule nchini kwa sababu ya udanganyifu. Hata hivyo, wanafunzi hao walipangiwa tarehe nyingine ya kurudia mitihani hiyo. Shule zilizofutiwa matokeo zilikuwa katika wilaya za Ubungo na Kinondoni jijini Dar es Salaam, Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza na Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma.Kwa mujibu wa Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde, uongozi wa Idara ya Elimu ya Chemba kwa kushirikiana na waratibu wa elimu na walimu wakuu walipanga kwa makusudi kufanya udanganyifu katika mitihani. Hata hivyo, Necta ilipotangaza matokeo ya mtihani wa kuhitimu darasa la saba 2018 ilibainisha kuwepo ongezeko la ufaulu kwa asilimia 4.96 tofauti na ufaulu wa 2017. Jumla ya watahiniwa 733,103 kati ya 943,318 wamefaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2018, ambapo wasichana ni 382,830 sawa na asilimia 77.12 na wavulana ni 350,273 sawa na asilimia 78.38.Takwimu zinaonesha ufaulu katika masomo ya Kiingereza, Maarifa ya jamii, Hisabati na Sayansi umepanda kwa asilimia kati ya 4.03 na 11.92 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia. Wakati huo huo, ufaulu katika somo la Kiswahili umeonekana kushuka kwa asilimia 1.44. Katika tyukio linghine la kumbukumbu ya mwaka 2018, Novemba 27, 2018 Rais John Magufuli anafungua rasmi maktaba ya kisasa na Kituo cha Kichina katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Katika ufunguzi huo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa William Anangisye anaelezea kuwa eneo la maktaba hiyo lina ukubwa wa ekari 4.7 na jengo limechukua mita za mraba 20,000.Maktaba hiyo ina maeneo ya kusomea yanayoweza kuhudumia wasomaji 2,100 kwa wakati mmoja. Ina eneo la wanafunzi wenye uhitaji maalumu na maeneo mengine mbalimbali ndani yake. Maktaba hiyo imejengwa kwa ufadhili wa Serikali ya China kwa gharama zinazokadiriwa kuwa Dola milioni 41.28. Mradi umejumuisha majengo mawili; moja ni la maktaba yenyewe na lingine ni Taasisi ya Confucius inayofundisha utamaduni na Lugha ya Kichina kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Watanzania wengine.Hii ni moja ya maktaba za kipekee kwani ina rafu zinazoweza kuchukua vitabu 800,000, na ndani ya maktaba hiyo kuna ukumbi unaoweza kuchukua watu 600. Kimsingi, mwaka 2018 unaoeleka ukingoni una mambo mengi chanya katika sekta ya elimu nchini Tanzania ambayo ni kumbukumbu na ufahari kwa Mtanzania likiwemo suala la kuongezeka kwa ubora wa elimu na idadi kubwa ya wanafunzi wanapohitimu na kufaulu kuongezeka.Haya likiwamo ongezeko la watoto wanaandikishwa kuanza darasa la kwanza ni sehemu ya matunda ya Sera ya Elimu Bure inayosimamiwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli ambayo, ina changamotio zake zinazozidi kutatuliwa, imekuwa mkombozi kwa Watanzania.
3
NAIROBI, KENYA NAIBU Rais wa Kenya, William Ruto, amemtaja Raila Odinga kama mwanasiasa asiye na demokrasia na mshamba kutokana na vurugu na ghasia zilizoshuhudiwa jijini alipopokelewa na wafuasi wake waliofurika katika barabara za jijini hapa  kumkaribisha kiongozi wao, lakini wakakabiliana na polisi waliokuwa wakiwazuia kufika kwenye bustani ya Uhuru ambako walipanga kuandaa mkutano mkubwa wa kisiasa. Akizungumzia hatua ya Jeshi la Polisi kuwasambaratisha wafuasi wake, Raila alilalamikia vitendo vya polisi kwa wafuasi wake na viongozi wa NASA, akishangazwa kwa nini viongozi hao wawili hawakuja kwenye uwanja wa ndege kukutana naye alipowasili kutoka Marekani. “Mmenisubiri kutoka asubuhi na ninasema asante. Mmeonyesha upendo mkubwa. Hasira yangu ni kwa huyu kijana mdogo Uhuru Kenyatta. Badala ya kuja kunikaribisha kwenye uwanja wa ndege, aliamua kukaa na naibu wake,” Raila alisema. Wakati msafara wa Raila ulipokuwa ukiingia jijini kwa takriban saa sita, magari kadhaa yaliharibiwa kwenye makabiliano hayo huku polisi wakitumia vitoa machozi, mawe na risasi kamili kuwazuia viongozi wa upinzani na wafuasi wao kufika jijini. Watu watano walipoteza maisha yao, huku wengine wengi wakipata majeraha tofauti kwenye makabiliano hayo.
2
Ramadhan Hassan -Dodoma RAIS Dk. John Magufuli amesema Serikali itaendelea kulipa mishahara ya walimu licha ya janga la ugonjwa wa corona  huku akimwaga ajira mpya 13526 katika kada hiyo. Kauli hiyo aliitoa jana Jijini hapa wakati akizungumza  katika Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ambapo Rais Magufuli alisema kada ya ualimu ni muhimu hivyo Serikali ya awamu ya tano itaendelea kutoa kipaumbele katika sekta hiyo. “Mmoja wa wanafalsafa mashuhuri duniani Aristotle  aliwahi kutamka maneno yafuatayo na naomba kumnukuu alitamka; ‘watu wanaotoa elimu au maarifa kwa watoto wanapaswa kuheshimiwa zaidi kuliko wazazi kwavile wazazi kazi yao ni keleta watoto duniani wakati wao wanatoa maarifa wanawapatia mbinu za kuishi duniani. “Waheshimiwa walimu kutokana na hatua ambazo tumechukua mafanikio mengi yametokea, uandikishaji wanafunzi umeongezeka mara dufu kwa wastani wanafunzi milioni moja kwa mwaka 2015 hadi kufikia milioni 1.6 kwa mwaka huu,”alisema. MISHAHARA LICHA YA CORONA Rais alisema licha ya changamoto ya ugonjwa wa corona, Serikali itaendelea kuwalipa mishahara hata kama ugonjwa huo utaendelea kuwepo kwa muda mrefu. “Nitumie fursa hii kuwashukuru walimu wote nchini kwa kuwezesha kupatikana kwa mafanikio haya ninawashukuru sana. Ndio maana tumeendelea kuwalipa mishahara yenu katika kipindi hichi licha ya shule kuwa zimefungwa. “Tukumbuke katika wafanyakazi wote tunaowalipa walimu ni zaidi ya 266,905 na katika mishahara ambayo tunalipa tunalipa karibia bilioni 600 kwa hiyo nusu ya mishahara bilioni 300 zinaenda kwa walimu. “Kwa hiyo unaweza ukajiuliza kila mwezi unatoa bilioni 300 kwa wafanyakazi ambao ni walimu ambao hawaendi kufundisha.Hii ni thamani kubwa kwa imani ya Serikali ya awamu ya tano kutambua  kazi kubwa inayofanywa na walimu. Napenda kuwahakikishia walimu wote nitaendelea kuwalipa mishahara kwa sababu Corona haijaletwa na walimu,”alisema Rais Magufuli. Alisema sekta hiyo ni muhimu na ndio ambayo imekuwa ikizalisha wataalamu katika sekta zingine hivyo Serikali yake itaendelea kuipa kipaumbele. “Sekta ya elimu ni zaidi ya  sekta  zote na nyie walimu ndio wazalishaji wa sekta hizo hivyo hatuna budi kutambua umuhimu wa sekta hii. Natambua kwamba changamoto bado zipo niwahakikishie walimu serikali inazifahamu na inaendelea kuzishughulikia,”alisema. Rais aliwahakikishia walimu nchini kwamba Serikali haiwezi kuwatupa kwani anazifahamu shida zote za walimu kwani na yeye amewahi kuwa mwalimu. “Sisi sote ni kitu kimoja na nataka niwahakikishie siwezi kuwatupa walimu wa Tanzania tunajenga nyumba moja ninafahamu shida za walimu kwa sababu hata mimi nimeishi, kuwakana walimu ni kujikana nafsi yangu jambo ambalo siwezi nikafanya ndugu zangu walimu.Kamwe hatupaswi kufanya kazi kwa uadui.”alisema Rais Magufuli. AUMWAGIA SIFA UONGOZI ULIOPITA Aidha,Rais alisema uongozi uliopita wa CWT umefanya kazi nzuri kwa kutetea maslahi ya walimu pamoja na kuwa kiunganishi kati ya Serikali na walimu. “Ninafahamu mkutano huu ni kuwapata viongozi wapya na sipendi kuonekana napiga chapuo ila ukweli lazima useme uongozi huu ambao unamaliza muda wake umejenga uhusiano mzuri sana na Serikali inayoiongoza na hili nasema kwa dhati sana. “Uongozi huu ambao umemaliza muda wake umejenga uhusiano mzuri na Serikali kwa kutatua changamoto na walikuwa wepesi kutafuta viongozi wa serikali kwa lengo la kujadiliana nao “Na ndio maana hamkusikia misuguano yoyote nakumbuka wakati tunafunga shule na vyuo kwa sababu  ya ugonjwa wa corona siku ya kwanza, kesho yake nikapigiwa simu ikawa inapiga mara nyingi na baadae ikapokelewa na wasaidizi wangu. “Wakaniambia  Rais wa Chama cha Walimu anataka kuongea na wewe, nikamsikiliza alichozungumza Mheshimiwa Rais kwa sababu sasa umefunga shule na vyuo inawezekana ukafunga kwa muda mrefu usifanye kama wanavyofanya nchi nyingine ukakata mishahara ya walimu. “Nikajiuliza nikakumbuka wakati wangu nikiwa mwalimu na bahati nzuri mmoja wa walimu aliyenifundisha Saikolojia mwalimu Luimbiza yupo hapa alinifundisha Mkwawa ila bado kijana tu hizi ndio faida za kuwa mwalimu. “Baada ya kuniomba hivyo nilitafakari na ndio maana baadae nikazungumza hata ingekaa mwaka mzima au miaka kumi sitafuta mishahara ya kuwalipa walimu hili, lisichukuliwe kama kampeni nimezungumza yale ya ukweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu kwahiyo msije mkampa kura eti kwa sababu aliwasemea,”alisema. UBORESHAJI SEKTA YA ELIMU Aidha, Rais Magufuli alisema wakati wa kampeni zake za mwaka 2015 na wakati akifungua Bunge aliahidi kuboresha sekta ya elimu kuanzia ngazi ya awali hadi Chuo Kikuu. Alisema katika hilo anafarijika kuona kipindi cha miaka mitano amefanikiwa  kutimiza ahadi hiyo. “Namshukuru Katibu Mkuu (Deus Seif) ametaja mambo ambayo tumeyafanya ikiwa ni pamoja na kutoa elimu bila malipo kuanzia shule ya msingi  hadi  sekondari sio kwamba wanasoma  bila malipo kinachofanyika ni serikali kubepa jukumu hilo kutoka kwa wazazi,”alisema. Alisema tangu  Desemba 2015 hadi Februari 2020 Serikali imetumia   zaidi ya shilingi trilioni 1.01 kugharamia elimu bila malipo. Pia, alisema wamefanikiwa kuongeza   idadi ya shule za msingi kutoka shule 16899 mwaka 2015 hadi kufikia shule  17804 mwaka huu na shule za sekondari zimeongezeka kutoka  4708 mwaka 2015 hadi kufikia shule 5330 mwaka 2020. “Pia tumekarabati shule kongwe za sekondari 73 kati ya 89, tumejenga mabweni 253 na nyumba za maabara 227, tumetoa vifaa kwenye maabara 2566 tumepunguza kiasi kikubwa tatizo la madawati ambapo idadi yake imeongezeka kutoka zaidi ya madawati milioni tatu mwaka 2015 hadi kufikia madawati zaidi ya milioni nane sawa ongezeko la zaidi ya asilimia 200,”alisema. Kwa upande wa Vyuo vya Ualimu, Rais Magufuli alisema wamekarabati    18 na kujenga vipya viwili katika maeneo Mutunguru na Kabanga. “Kali kadhalika tumepeleka Computer 1550 kwenye vyuo vyote 35 kwa lengo la kufundisha masomo ya Tehama. “Tumeongeza Vyuo vya Ufundi (Veta) kutoka 672 mwaka 2015 hadi kufikia 712 mwaka  2020 tumekarabati pamoja na  vifaa na miundombinu ya kufundishia katika vyuo  54 vya Maendeleo ya Jamii na pia  tumejenga hosteli, kumbi za chakula kwenye Vyuo Vikuu,”alisema. Pia, alisema  wameongeza    bajeti ya mikopo ya elimu ya juu kutoka  shilingi bilioni 341 mwaka 2014-2015 hadi kufikia shilingi bilioni 450 mwaka 2019 -2020 KUPANDISHA VYEO Vilevile, alisema Serikali tayari imewapandisha vyeo watumishi 306917 ambapo walimu ni 106367 na mwaka huu inatarajia  kuwapandisha vyeo watumishi 290625 wakiwemo walimu  166548. “ Ninaimani kuwa miongoni mwao walimu wenye sifa waliotarajiwa na wale waliopandishwa vyeo mwaka 2013-2014.
3
TIMU ya Taifa ya Soka ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kushuka dimbani leo ugenini kuikabili Sudan katika mchezo wa kufuzu fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan 2020).Mchezo huo utachezwa ugenini kuanzia saa 1:00 usiku, huku Stars ikiwa imetoka kupoteza mchezo wa kwanza bao 1-0 uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ni mchezo muhimu kwa Taifa Stars kuhakikisha inapata matokeo ya ushindi kuanzia mabao 2-0 na kuendelea ili kupata nafasi ya kufuzu kwa mara ya kwanza baada ya miaka 10 Tanzania ilipofuzu kwa mara ya kwanza mashindano hayo yalipofanyikia Ivort Coast.Timu hizo zina historia mara ya kwanza katika michuano kama hiyo ya kufuzu zilikutana Dar es Salaam na Stars kushinda 3-1 kisha ziliporudiana Stars ikashinda tena 2-1 ugenini. Lolote linawezekana kama tu Stars itakuwa imejipanga vizuri dhidi ya mpinzani wake huyo. Beki wa Stars, Erasto Nyoni alisema maandalizi yako vizuri na anaamini watapata matokeo mazuri.“Sisi tuko salama hakuna mtu mwenye majeruhi na tumejiandaa vizuri, kikubwa ni Watanzania kutuombea heri tupate matokeo mazuri,”alisema.Stars kabla ya kuvaana na Sudan ilicheza mchezo mmoja wa kirafiki dhidi ya Rwanda ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo huo ambapo licha ya kutoka suluhu Kaimu Kocha Mkuu Ettiene Ndayiragije aliwatumia wachezaji wengi wa ndani kuwapa mazoezi.Katika michezo iliyopita safu ya ushambuliaji ilionekana kuwa butu kwa kutengeneza nafasi nyingi na kushindwa kufunga, lakini ameongezwa mshambuliaji mpya Ditram Nchimbi hivyo, huenda mambo yakawa mazuri. Sudan imekuwa ikicheza mchezo wa kujilinda na mashambulizi ya kushtukiza na ilifanya hivyo katika mchezo wa kwanza labda watacheza kwa kufunguka zaidi leo. Timu hizi zimekutana baada ya Stars awali kuwatoa Kenya.
3
WIZARA ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ya Zanzibar imesema njia pekee ya wakulima kupiga hatua kubwa ya uzalishaji wa mpunga ni kutumia kilimo cha umwagiliaji.Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Rashid Ali Juma alisema kilimo cha umwagiliaji ndio mkombozi wa wakulima ambao kwa sasa wanaweza kulima muda wowote mwaka mzima. Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa sasa inatekeleza mradi mkubwa wa umwagiliaji maji mashambani ambao ni fedha za mkopo kutoka Benki ya Exim ya Korea ya Kusini.‘’Serikali tayari inatekeleza mradi mkubwa wa umwagiliaji maji mashambani ambao unatekelezwa na wenzetu Benki ya Exim kutoka Korea ya Kusini ikiwa ni mkopo,’’ alisema. Juma alisema mradi huo wa umwagiliaji ulianza Desemba, 2018 ambapo kazi kubwa ni ujenzi wa mitaro ya kupitishia maji inayoenda mashambani pamoja na kujenga pia njia zake.Aidha, alizitaja kazi nyingine zitakazofanyika ni kuchimba visima vya uzalishaji wa maji 49 vitakavyotumika kusambaza maji mashambani na ujenzi wa mabwawa manne ya maji. ‘’Hizo ndiyo kazi zitakazofanyika katika utekelezaji wa mradi wa umwagiliaji maji mashambani wenye lengo la kukuza uzalishaji wa mpunga kwa wakulima wetu, ‘’ alisema.Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Ahmada Kassim Haji alisema kama wakulima wa mpunga watajikita zaidi katika uzalishaji wa mpunga kwa umwagiliaji maji, yapo matumaini makubwa ya kujitosheleza kwa chakula. Alisema kilimo cha mpunga cha kutegemea mvua hakina uhakika kupata mavuno mazuri. ‘’Serikali imejikita katika kuimarisha kilimo cha umwagiliaji maji mashambani ambacho matarajio ni kukomboa wanawake, ‘’alisema.
3
KINSHASA, DRC UPINZANI umepanga kutumia nguvu ya umma baada ya Taume ya Uchaguzi nchini hapa kusema uchaguzi wa rais atakayechukua nafasi ya Rais Joseph Kabila hauna uwezekano wa kufanyika mwaka huu. Hilo huenda likazua upya machafuko yaliyoshuhudiwa mwaka jana kwa vile bi ukiukaji wa makubaliano yaliyoyasitisha mwaka jana, ambayo yalimruhusu Kabila kuendelea kubaki madarakani hadi mwishoni mwa mwaka huu. Kugoma kwa Kabila kuondoka madarakani mwishoni mwa muhula wake wa pili Desemba mwaka jana kuliibua machafuko yaliyoua makumi ya watu. Upinzani haukuchukua muda kuibuka kulaani tangazo hilo la Rais wa Tume, Corneille Nangaa, ikisema huko ni ‘kutangaza vita.’ “Rasilimali tulizo nazo, zinatupa sababu zaidi za kuamini kuwa Desemba, haitawezekana kufanyika uchaguzi kama ilivyopangwa,” Nangaa alisema katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa, TV5Monde. Chini ya makubaliano yaliyofikiwa Desemba 31 mwaka jana kati ya wawakilishi wa Kabila na viongozi wa upinzani, Kabila, aliye madarakani tangu 2001, pia alizuiwa kujaribu kubadili katiba ili awanie urais kwa muhula wa tatu. Hata hivyo, Kabila alisema uchaguzi utafanyika tu pale tume ya uchaguzi itakapomaliza kuorodhesha mamilioni ya wapiga kura. Katika kuitikia kauli za Nangaa, kiongozi wa upinzani Felix Tshisekedi aliandika katika mtandao wa Twitter kuwa rais wa tume ametangaza vita kwa watu wa Kongo na ameonya watachukua hatua kali kushirikisha nguvu ya umma mitaani.
2
SIMBA rasmi imemrejesha kundini Ibrahim Ajibu akitokea Yanga na usajili huo unaonekana kumkuna beki wa zamani wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo.Ajibu amesaini mkataba wa miaka miwili wa kucheza kwenye kikosi cha mabingwa hao wa Tanzania msimu ujao. Usajili huo unaonekana kumkosha Kihwelo aliyesema kuwa hakuna mchezaji wa kumuweka benchi Ajibu kwenye kikosi cha Simba.“Nikwambie tu hapa nchini hakuna wachezaji wenye vipaji kuwazidi Haruna Moshi ’Boban’ na Ibrahim Ajibu. Hata Samatta hana kipaji kikubwa kama Ajibu sema anajitambua tu,”alisema Kihwelo maarufu kama Julio.Julio ambaye pia amewahi kuwa kocha msaidizi wa Simba, alisema anafahamu vizuri Ajibu na kwamba akiondoa tabia yake ya uvivu wa mazoezi basi atafika mbali.“Wakati mimi na Kibadeni tukifundisha Simba, Ajibu alikuwa Simba B, nilipoenda Mwadui nilimchukua Ajibu na akatufungia mabao 26 tukapanda Ligi Kuu,” alisema Kihwelo.Aidha, Kihwelo alitilia shaka nyota wapya wa timu hiyo kutoka Brazil na kusema kuwa haamini kama mchezaji mwenye uwezo mkubwa tangu taifa hilo kubwa katika soka anaweza kuja kucheza Tanzania.Ajibu anarejea Simba baada ya kuondoka klabu hiyo na kujiunga na wapinzani wao wakubwa Yanga misimu miwili iliyopita.Anarejea Simba akiwa kwenye kiwango bora baada kuhusika kwenye mabao 22 ya Yanga akiwa amefunga mabao sita na kutengeneza 15.
4
ELIZABETH HOMBO-DAR ES SALAAM NI masikitiko. Ndivyo unaweza kusema baada ya Jeshi la Polisi, kueleza namna Hamisi Luwongo, ambaye anashikiliwa kwa tuhuma za kumuua mkewe, Naomi Marijani, alivyofanya mauaji hayo na baadaye kuteketeza mwili wake kwa moto. Inadaiwa Naomi  alitoweka katika mazingira ya kutatanisha Mei mwaka huu, ambapo picha na taarifa zilizodaiwa kuandaliwa na mumewe Luwongo, zilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikidai atakayefanikisha kupatikana kwake, atapa zawadi ya Sh milioni moja. Akizungumza na MTANZANIA jana ofisini kwake, Kamanda Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Amon Kakwale,  alisema Mei 19, Luwongo alifika katika Kituo cha Polisi Gezaulole, Kigamboni na kufungua jalada la taarifa kuwa mkewe, Naomi ametoroka. Alisema kama ilivyo taratibu za Polisi walianza uchunguzi ambapo Juni 12, Luwongo alifika tena kituo hicho cha polisi na kueleza kuwa Naomi ametelekeza mtoto anayeitwa Grecious mwenye umri wa miaka saba. Kamanda huyo alisema baada ya Jeshi la Polisi kupokea taarifa hizo, kesi hizo zilianza kufanyiwa kazi. Alisema wakati wanaendelea na uchunguzi juu ya suala hilo, ndugu wa Naomi nao walifika katika kituo cha Polisi Chang’ombe, wakieleza kuwa ndugu yao alikuwa amepotea na wana shaka na mumewe kuhusu kutoweka kwake. Alisema kutokana na maelezo hayo ya ndugu wa Naomi, Jeshi la Polisi likamtia mbaroni Luwongo kwa ajili ya mahojiano. Kamanda Kakwale alisema Julai 15, akiwa mbele ya jeshi hilo akaeleza kuwa taarifa alizokuwa ameeleza awali hazikuwa za kweli na kwamba akaanza kueleza ukweli wa namna mkasa mzima ulivyokuwa. “Luwongo alilieleza Jeshi la Polisi kwamba walikuwa na ugomvi na mkewe ambapo siku hiyo asubuhi wakati Naomi anatoka kumpeleka mtoto shule, kukatokea ugomvi ambao ulisababisha umauti. “Akaeleza kuwa baada ya kubaini kwamba amepoteza uhai alichukua mwili mpaka kwenye banda la kuku, ambapo aliweka magunia mawili ya mkaa na kuweka mafuta ya taa na kuwasha moto. “Katika maelezo yake hayo, akaendelea kueleza kuwa baada ya kuhakikisha kwamba mwili wote umeungua moto akachukua mifupa na kuweka kwenye gari lake na kwenda nayo katika shamba lake huko Mkuranga mkoani Pwani. “Alipofika katika shamba lake hilo akachimba shimo na kufukia na akapanda mmea wa mgomba juu yake,”alisema Kamanda Kakwale Aidha, kamanda huyo aliendelea kueleza kuwa baada ya taarifa hizo za Luwongo timu ya Jeshi la Polisi wakaongozananaye kwenda Mkuranga. “Walipofika Mkuranga akaonyesha mahali ambapo amechimba shimo na timu hiyo ikabaini mabaki na mifupa na wakayachukua na tayari wamekabidhiwa kwa wenzetu wa kitengo cha sayansi kwa ajili ya kufanyiwa kipimo cha DNA,”alisema. Alisema hatua inayofuata sasa ni kuhakikisha wanapata matokeo ya DNA ambapo itachukuliwa damu ya mtoto au ya ndugu wa Naomi ili waweze kuamini kuwa mabaki hayo ni ya marehemu. “Baada ya matokeo hayo sasa jalada litaenda kwa AG (Mwanasheria Mkuu wa Serikali) halafu yeye atalifikisha mahakamani na mtuhumiwa atajibu tuhuma hizo,”alisema. Akizungumzia kuhusu chanzo cha ugomvi, Kamanda Kakwale, alisema ni wivu wa mapenzi ambapo kulikuwepo kutoaminiana baina ya wanandoa hao. Aidha alitoa wito kwa Watanzania kuwa pale wanapopata taarifa kuwa mtu fulani amepotea wasiishie tu kusema kuwa ametekwa na watu wasiojulikana bali watoe fursa ya kujiridhisha.
0
NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Dylan Kerr, ameanza kujivunia kikosi chake kuwa kwa sasa kipo imara na kinaweza kumpatia matokeo mazuri kwenye mechi zilizobakia za Ligi Kuu Tanzania Bara kama ilivyokuwa mkakati wake. Simba hivi karibuni ilifanikiwa kuifunga Kimbunga FC ya Zanzibar kwa mabao 5-2, ikiwa ni mchezo wao wa kwanza wa majaribio tangu ligi isimame, kesho itajipima tena na timu nyingine visiwani humo. Akizungumza na MTANZANIA jana, Kerr alisema kadiri siku zinavyokwenda timu yake inazidi kuimarika hivyo kuendelea kumpa matumaini kuwa malengo aliyojiwekea na makubaliano yake na uongozi ya kuifikisha timu nafasi ya pili yatatimia. “Nina timu nzuri na imara, wachezaji wote wanajitambua na wanatambua majukumu yao, wanajua nini nataka na wanatekeleza yote hata kama kuna mapungufu, basi ni machache,” alisema. Mwingereza huyo alisema anafurahishwa na kiwango cha kila mchezaji kwenye timu yake kwa sasa, kwani kila mmoja ameweza kuonyesha uwezo wake jambo ambalo analifurahia. Naye kwa upande wake, ofisa habari wa klabu hiyo, Haji Manara, alisema bado wanaangalia timu watakayojipima nayo kesho ambapo hadi leo timu hiyo itakuwa imefahamika na tayari kwa kucheza nayo. “Tunachagua timu kulingana na uhitaji wa mwalimu, hivyo kama atahitaji zaidi tutamtafutia lakini kwa sasa amehitaji mechi hizo mbili na tayari moja ameshaipata na hii ya pili watacheza Jumanne (kesho),” alisema. Simba inayoshika nafasi ya nne kwenye ligi ikiwa na pointi 21, imeweka kambi visiwani humo ikiwa ni mahususi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo ujao wa ligi dhidi ya vinara Azam FC, utakaofanyika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam Jumamosi hii.
4
Mkutano huo ambao pia kampuni 50 za Ufaransa zitashiriki zikiwamo kampuni kubwa kama Total, Airbus, Sogea Satom na Alstom, kutakuwa na majadiliano mbalimbali kati ya wafanyabiashara wa Ufaransa na Tanzania ili kuona wapi taifa hilo linaweza kushiriki katika uwekezaji.Taarifa ya kuwapo kwa mkutano huo ilitolewa na Balozi wa Ufaransa nchini, Malika Berak wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Ufaransa inayoanza Jumatatu, Aprili 3 hadi 6, mwaka huu.Alisema Wiki ya Ufaransa ambayo itafanyika kwa mara ya kwanza nchini katika Makumbusho ya Taifa, imelenga kuimarisha uhusiano wa biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Ufaransa, ambao kwa sasa wanafanya biashara inayofikia Euro milioni 200 kwa mwaka huku anayeingiza sana akiwa ni Ufaransa.“Nia ya tukio hili ni kuitangaza Tanzania kwa wawekezaji wa Ufaransa ambao nao watataka kujua kwamba wanaweza kushiriki wapi kwa kuzingatia mahitaji,” alisema Balozi Berak na kuongeza kuwa pamoja na kuonesha uwezo, kutakuwa na mawasilisho mbalimbali yanayohusu uwezo wa kampuni za Kifaransa katika sekta za nishati, nishati mbadala, usafirishaji, Tehama, na ujengaji uwezo kwa wafanyabiashara au wawekezaji binafsi nchini.Aidha, wiki hiyo itakuwa na mazungumzo kati ya watendaji wa serikali, wafanyabiashara hao wa Ufaransa na wa hapa nyumbani, makongamano na maonesho.Pamoja kuwepo kwa mabalozi hao ambao wananakuja kujifunza kuhusu Tanzania na Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza ikiwa ni kuongeza wigo wa uelewa wa siasa za Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla, kutakuwa na wataalamu wa masuala mbalimbali kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Maendeleo ya Kimataifa ya Ufaransa, Shirika la Misaada la Ufaransa na watendaji wa kampuni kubwa za Ufaransa na washirika wao.Kwa kuzingatia aina ya watu watakaokuwepo, Balozi Berak alisema wiki hiyo itakuwa ni wiki ya Watanzania kujifunza na kuelewa wanachoweza kukivuna kutoka Ufaransa kwa ajili ya maendeleo ya viwanda na kuibadili nchi kutoka kutegemea bidhaa za kilimo hadi viwanda.
5
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wameendeleza ushindi katika mchezo wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara baada ya kushinda mabao 3-0 dhidi ya African Lyon.Katika mchezo huo uliochezwa jana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha, mabao ya Simba yalifungwa na John Bocco mawili na Adam Salamba aliyefunga bao moja.Ushindi huo unaifanya Simba kubaki katika nafasi ya tatu kwa kufikisha pointi 42 katika michezo 17 huku wapinzani wake African Lyon wakiendelea kushika mkia kwa pointi 21 katika michezo 27 iliyocheza.Katika mechi ya jana, kipindi cha kwanza timu zote ziliingia kwa kasi kila mmoja akionesha kutaka ushindi na dakika ya nne, Lyon ilipata nafasi na kushindwa kuitumia kupitia kwa Steven Mwasyika na dakika 20, Rashid Juma wa Simba alipata nafasi ya wazi na kushindwa kuitumia.Dakika 28 wekundu hao walipata bao la uongozi la mkwaju wa penalti baada ya Rolland Msonjo wa Lyon kushika mpira eneo la hatari na bao likafungwa na nahodha Bocco.Bao la pili lililofungwa na Salamba dakika ya 44 lilitokana na kipa wa Lyon kupangua shuti lililopigwa na Bocco kabla Salamba hajauwahi na kuujaza wavuni.Lyon licha ya kujitahidi kucheza walikuwa wanashindwa kuingia ndani ya eneo la hatari la Simba kutokana na ukuta mkali wa mabingwa hao watetezi.Bocco aliifungia Simba bao la tatu sekunde chache baada ya kuanza kipindi cha pili akiunganisha krosi ya Rashid Juma.Katika mechi hiyo, Simba ndiyo ilimiliki mpira kwa asilimia kubwa.Kocha wa Simba, Patrick Aussems aliwapumzisha baadhi ya nyota wa kikosi cha kwanza waliocheza mchezo uliopita dhidi ya Yanga isipokuwa Aishi Manula, Pascal Wawa na Bocco ili kuwapa nafasi wale waliokuwa hawapati na wengine kuandaliwa kwa mechi ijayo dhidi ya Azam.Michezo mingine iliyochezwa jana ni Azam FC iliyolazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Coastal Union, Mwadui ilishinda 2-1 dhidi ya Biashara na Ruvu Shooting ikitoka suluhu dhidi ya Kagera Sugar.
4
NA OSCAR ASSENGA, KOROGWE. TATIZO la uhaba wa nyumba za walimu wilayani Korogwe mkoani Tanga, limesababisha walimu kushindwa kuishi  kwenye shule wanazopangiwa kutokana na miundombinu kutokuwa rafiki. Hayo yalisemwa juzi na Kaimu Ofisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Korogwe, Martha Kusare, wakati wa upokeaji majengo matatu ya maabara yaliyojengwa na Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Vuga Development Initiative ya mkoani Arusha, ikishirikiana na A Better World kutoka nchini Canada kwa Shule ya Sekondari ya Patema iliyopo Kata ya Mpale. Alisema hali hiyo imekuwa kikwazo kikubwa cha wanafunzi kushindwa kufikia malengo yao ya kitaaluma na kuiomba Serikali kuona namna bora ya kuanzisha ujenzi wa nyumba za walimu kwenye maeneo ya vijijini, kwani kuna uhaba mkubwa kutokana na kukosekana hata nyumba za kupangisha. Alisema kitendo cha kukosekana kwa nyumba za walimu kwenye maeneo ya shuleni kumechangia hata kuwapo kwa tatizo la utoro wa wanafunzi wao na hivyo kama halmashauri wamejipanga kukabiliana nalo kwa vitendo ili kulimaliza. “Ukiangalie hivi sasa walimu wanaopangiwa maeneo ya vijijini wanafika kuripoti na kukaa kwa miezi kadhaa na wanapoona hakuna mazingira mazuri, wanalazimika kuhamia maeneo mengine, kitendo ambacho ni hatari kwa maendeleo ya sekta ya elimu,” alisema. Hata hivyo, alisema wanaishukuru watu wa Canada kwa kushirikiana na Vuga kusaidia kumaliza nyumba ya mwalimu shuleni hapo. Naye Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Azidu Kaoneka, alisema umaliziaji wa maabara hizo, nyumba  moja  ya walimu na kuwawekea kifaa cha kuzalisha umeme kupitia jua (mobisol), vimegharimu Sh milioni 75.  
3
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zuberi Maulidi amesema atafi kisha kwa Rais John Magufuli madai ya kuwepo kwa sintofahamu, juu ya malipo ya baadhi ya wakulima wa korosho, ambao wamerejeshewa mazao yao baada ya uhakiki.Maulid ambaye pia ni mlezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mikoa ya Lindi na Mtwara, ametoa ahadi hiyo baada ya viongozi wa CCM wa Mkoa wa Mtwara, kudai kuwa baadhi ya wakulima wa korosho, walifanyiwa uhakiki na kupewa stakabadhi ya malipo, lakini baadaye walirejeshewa korosho, bila kupewa taarifa kama watalipwa au la.Viongozi hao wa CCM walisema hayo mkoani hapa hivi karibuni, wakati wa vikao vya ndani na nje vya CCM katika ziara ya mlezi huyo wa chama.Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mtwara, amesema kuna zaidi ya tani 160 zimerudishwa kwa wakulima katika vyama vya msingi vya Mtungulu na Lengo wilaya ya Newala.Zimerejeshwa kwa madai ya kukosa ubora wakati uhakiki ulishafanyika na wakulima kupewa stakabadhi ya malipo.Maulidi aliwasili wilayani Masasi mkoani hapa na kuanza kukagua shughuli za chama na miradi mbalimbali ya maendeleo.Katika ziara hiyo, viongozi hao wa CCM walimuomba mlezi huyo aingilie kati malipo ya korosho, ambayo yameonekana kuwa na changamoto kwa wakulima wa Mkoa wa Mtwara, hatua iliyomfanya Spika huyo kuahidi kulifikisha kwa Rais Magufuli.“Tunafahamu kuwa kero hii ni kubwa hapa Mtwara, suala la korosho ni kila kitu kuanzia siasa, linagusa uchumi na masuala nyeti kama usomeshaji wa watoto, ujenzi wa nyumba bora, uimarishaji wa miundombinu na masuala yote muhimu.“Niwaahidi na niwahakikishieni kuwa malalamiko yenu nimeyapata kwa ukamilifu na naahidi kuyafikisha kwa Mwenyekiti wetu wa Taifa (Rais Magufuli) na naahidi kwamba nikitoka hapa nakwenda kuyafikisha na ninataka nimfikishie kwa mkono wangu na kumhadithia kwa mdomo hali niliyoikuta.“Hofu yangu ni nani huyo anayesema mkulima wa korosho arudishiwe bila kumwangalia aliyepokea? Ni nani aliyesababisha korosho iwe chafu ni mkulima au aliyepokea, maana mkulima alikuwa tayari ana stakabadhi ya malipo mkononi,” amesisitiza Maulid.Amesema, zao la korosho katika Mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma, ndilo linatengeneza siasa na ndiyo uchumi, elimu, matibabu, barabara na kila kitu. Hivyo,Alisema haitakubalika kuona zao hilo linachafua mipango mizuri ya utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kuwaletea wananchi maendeleo.
3
WAZAZI wametakiwa kuwa makini baada ya ugonjwa wa kisukari kuongezeka miongoni mwa watoto na vijana jambo ambalo wataalamu wameainisha dalili ambazo wanapaswa kuzifahamu mapema wawafikishe hospitalini.Miongoni mwa watoto wenye ugonjwa huo ni wenye umri wa mwaka mmoja huku dalili zinazotajwa mara nyingi kukumba kundi hili ni tano ambazo ni hatari zaidi ikiwemo ya kukojoa usiku kitandani kwa mtoto aliyeacha kukojoa, kuamka mara nyingi usiku kwa ajili ya haja ndogo, kukojoa mara kwa mara, mkojo mwingi na kiu ya mara kwa mara.Hayo yalielezwa hivi karibuni na wataalamu wakiwamo viongozi wa Chama cha Kisukari Tanzania (TDA) na Shirikisho la Magonjwa yasiyo ya Kuambukiza (TANCDA) katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi. Mwenyekiti wa TDA, Profesa Andrew Swai alitaja dalili nyingine za kisukari kwa watoto na vijana walio katika balehe ni kula sana, kupungua uzito na kuchoka sana.“Lakini pia mara chache wanaweza wakawa wanaumwa mara kwa mara magonjwa kama vile fangasi za sehemu mbali mbali za mwili,” alisema.Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali ya Hindul Mandal ambaye pia ni Katibu Mkuu wa TDA, Dk Kaushik Ramaiya alikiri kuwapo ongezeko la watoto wenye kisukari akishuhudia kuwa miongoni mwa waliofikishwa hospitalini kwake wapo wenye umri wa mwaka mmoja.Wakati awali ugonjwa wa kisukari ulichukuliwa kuwa unaathiri watu wazima pekee, wataalamu hao wamefafanua kwamba inawezekana zamani watoto wengi walikuwa hawapimwi au walikuwa hawapati tiba sahihi ya kisukari kwa hiyo tatizo halikuweza kuonekana kirahisi.Profesa Swai alisema haikufikiriwa kama watoto wadogo pia hupata kisukari hivyo nguvu kubwa ilielekezwa kwa watu wazima.Alisema upo uwezekano mkubwa kwamba watoto walikuwa wakifariki bila kujulikana au wakawekwa kwenye makundi ya magonjwa mengine kama vile malaria na pneumonia.Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kuwa idadi ya watu wenye kisukari imeongezeka kutoka milioni 108 mwaka 1980 na kufikia watu milioni 422 mwaka 2014.Kama akutakuwa na juhudi za kupambana na ugonjwa huo, shirika linasema ifikapo mwaka 2035, kutakuwa na wagonjwa milioni 592 duniani.Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu alisema juzi kuwa lengo la serikali ni kupunguza wagonjwa wa kisukari nchini kwa asilimia 28 ifikapo mwaka 2025 kwa kuweka mikakati mbalimbali ya kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.Takwimu za miaka sita iliyopita za Shirikisho la Kimataifa la Kisukari (IDF) zilikadiria kwamba kulikuwa na watoto 500,000 wenye chini ya umri wa miaka 15 duniani waliokuwa wakisumbuliwa na kisukari.Nchi zinazoongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha kisukari miongoni mwa watoto na asilimia kwenye mabano ni Ulaya (76) huku nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara zikiwa na kiwango kidogo cha asilimia nane.
3
KOCHA Mkuu wa timu ya Yanga, Mwinyi Zahera ameibuka na kusema kuwa Bodi ya Ligi inamuonea kwa kumfungia kuingoza timu yake katika mechi tatu, kwani yeye aliiomba mechi yao na Ruvu Shooting kusogezwa mbele ili kupata muda wa maandalizi baada ya mchezo wa kimataifa.Yanga ilicheza na Township Rollers nchini Botswana na kushinda 1-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Afrika, na Zahera alitaka mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu dhidi ya Ruvu Shooting kusongezwa mbele, ombi ambalo halikukubaliwa.Mbali na kufungiwa mechi tatu, pia kocha huyo amelimwa faini ya sh 500,00 kwa madai ya kutovaa mavazi nadhifu wakati walipocheza dhidi ya Ruvu Shooting na kuipa Yanga onyo kwa kushindwa kuhakikisha kocha wao anakuwa nadhifu.Alijitetea kuwa alivaa kaptula katika mchezo wao huo baada ya kubanwa na ratiba na kushindwa kurudi nyumbani kubadili nguo.Akizungumza jana jioni mara baada ya kutua kwenye Kiwanja cha Ndege cha Mwanza, Zahera alisema Bodi ya Ligi imemtafutia sababu tu, kwani kama kuomba mechi kusogezwa mbele, mbona kuna timu ilikuwa na viporo hadi 16 msimu uliopita, na iliomba mechi zake kusogezwa mbele, na ilikubaliwa.Akizungumza kuhusu mavazi, alisema mbona anavaa kama makocha wengine, wala haoni kama hilo ni tatizo.“Wakati wenzangu wanatoka pre-match meeting saa sita na nusu mchana waliniletea taarifa kwamba sitakiwi kuvaa kaptula nikawajibu mimi nimetoka Botswana nikapitiliza kambini mmoja kwa mmoja na sikurudi kwangu hivyo nikakosa muda wa kubadilisha nguo, ’’ Zahera.Hatahivyo, alisema kukosekama katika benchi la timu yake mechi tatu, hakutaharibu kitu, kwani anaimani na msaidizi wake kuisaidia timu yake kufanya vizuri katika mechi hizo, ambazo yeye atakuwa hayupo.Alisema aliposafiri katika majukumu ya timu ya Taifa (Congo), kocha msaidizi alisaidia timu yake kupata matokeo kwa kushinda mechi nne katika michezo mitano ya Ligi Kuu, ambapo Yanga ilipoteza mechi moja tu dhidi ya Lipuli msimu uliopita.Kocha huyo alisema timu yake ikiwa hapa, itacheza michezo ya kirafiki dhidi ya Pamba na Toto Africans, ambapo kambi hiyo itawasaidia sana.
4
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amefunguka kuhusu utendaji wa jeshi hilo katika miaka minne ya uongozi wa Rais John Magufuli, akimmwagia sifa kwa kuliimarisha, hali iliyolisaidia kudhibiti uhalifu nchini.Mbali ya hilo, ameeleza kuhusu anavyonyimwa usingizi na suala la ugaidi nchini Msumbiji, lakini pia alizungumzia mauaji ya mifugo wilayani Tarime mkoani Mara.Pia, amezungumzia suala la aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu (Chadema) kurejea nyumbani, kauli yake kuhusu vifo vya Akwilina Akwiline na David Mwangosi na madai kuwa hatoshi katika wadhifa huo.IGP Sirro amefanya mahojiano maalumu na gazeti hili na kutumia dakika 45 kuzungumza mambo hayo na mengine, akimpongeza Rais Magufuli kwa kipindi cha miaka minne kuwa ameweza kuliimarisha jeshi hilo.Alisema pamoja na changamoto ikiwemo matukio ya ugaidi yanayoendelea nchini Msumbiji kumnyima usingizi, Amiri Jeshi Mkuu Rais Magufuli amekuwa bega kwa bega na jeshi hilo.Alisema katika kipindi cha miaka minne, Jeshi la Polisi limekuwa imara zaidi, kuna mambo ambayo Rais Magufuli ameyafanya ambayo hayajawahi kufanywa kwa muda mrefu.“Sisi hatujawahi kununuliwa helikopta tangu enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, lakini Rais Magufuli ameweza kutoa shilingi bilioni 5.3 za kununua helikopta mpya inayotusaidia katika operesheni zetu,” alisema IGP Sirro.Alisema pia jeshi hilo lilikuwa na changamoto ya sare kwa askari wake na ilifikia kipindi askari wanaazimana sare na wengine kuuziana, lakini Rais Magufuli amelipatia jeshi hilo Sh bilioni 10 kwa ajili ya sare.Alisema Chuo cha Polisi Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam ni cha muda mrefu na kwamba awali kilikuwa chini ya jeshi baadaye wakapewa Polisi.Alisema chuo hicho kilikuwa cha mbao na kimechoka, lakini sasa wamejenga majengo mawili ya ghorofa mbili baada ya Rais Magufuli kuwapatia Sh milioni 700.“Vitu vingi sana ametuboreshea na kuhakikisha jeshi linafanya kazi kwa weledi, mkitaka kujua jeshi letu lipoje angalia matokeo ya Kibiti na Rufiji, mpaka Mtwara,” alisema mkuu huyo wa Jeshi la Polisi.“Hali ingekuwa mbaya si unaona Msumbiji wamepeleka mpaka Warusi kwenda kusaidia, kwa hiyo unaweza kutofautisha jeshi letu la Polisi na majeshi mengine, kwa sababu ya mkono wa Amiri Jeshi Mkuu na maelekezo yake, hakupenda kuona watu wake wapate matatizo, imesaidia kwa kiasi kikubwa” alisema.Alisema pia Rais Magufuli alilipatia jeshi hilo Sh bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa nyumba za Polisi nchi nzima.Ugaidi Msumbiji wamnyima usingizi IGP Sirro alisema mauaji yanayoendelea nchini Msumbiji na utekaji wa vijiji nchini humo, vinamnyima usingizi, kwani wanaofanya vile wengi wanatoka Tanzania.“Mashaka yangu ni kuwa wale walioenda Msumbiji watakuja kutusumbua, intelijensia yetu na wale tuliowakamata wanasema wanaenda Msumbiji kujiimarisha kisha warudi,” alisema IGP.Alisema jeshi lake limeshawakamata watu 104 wanaoshukiwa kuwa waasi, wanaopanga kuanzisha ngome yao katika taifa jirani la Msumbiji.Aidha, alifafanua kuwa jeshi la polisi limeanzisha operesheni dhidi ya wahalifu Mashariki na Kusini mwa nchi na baadhi ya washukiwa walikamatwa, wengine walikufa na wenginewalitoroka.“Washukiwa waliokamatwa walipohojiwa wamesema walikuwa wanakwenda Msumbiji kujiunga na makundi ya wapiganaji wenye misimamo mikali.“Mashambulizi takriban 40 yamefanyika tangu Oktoba mwaka jana katika Jimbo la Cabo Delgado nchini Msumbiji ambalo liko mpakani na Tanzania. Zaidi ya watu 100 wameuawa katika mashambulizi hayo, wasiwasi wangu kule wanajenga ‘base’, watarudi, inabidi tujizatiti hasa na hilo ndilo linalonikosesha amani,” anasisitiza.Wizi wa mifugo Tarime Alisema matukio mengine yanayomnyima usingizi ni wizi wa mifugo wilayani Tarime Mkoa wa Mara, ambayo mingi inaenda Kenya.IGP Sirro anasema jeshi hilo ni lazima wafanye mkakati kudhibiti, kwani mtu anapoibiwa ng’ombe watano ni kumuingiza kwenye umaskini.Aonya maandamano wakati wa uchaguzi Alisema kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 24, mwaka huu na Uchaguzi Mkuu wa 2020, wameimarisha jeshi vizuri. Alisema hawatapuuza uchaguzi uwe mdogo au mkubwa na kwamba wamejipanga vizuri.Alisema kila mkoa wameweka madawati ya uchaguzi, ambayo yanatoa elimu na pili wale wachache watakaovunja sheria watawashugulikia.“Sasa tunakwenda katika uchaguzi, hatuwezi kupuuza, ili tuweze kwenda vizuri lazima kuwa na mpango mkakati wa kuzuia na kupambana na wale watakaoleta uhalifu wa kuvuruga,” alisema IGP Sirro.Aliongeza, “Angalizo kuna watu bila kufanya fujo, bila kuleta ujanja ujanja hawawi na amani, tutawashugulikia na askari wameshajipanga na wana vifaa vya kisasa.“Tumejiimarisha vizuri na sisi hatupuuzi uchaguzi uwe mdogo au mkubwa, tumejipanga vizuri na kila mkoa tumeweka madawati ya uchaguzi; kwanza kutoa elimu na pili wale wachache watakaovunja sharia tutawashughulikia.“Angalizo kuna watu bila kufanya fujo, bila kuleta ujanja ujanja hawawi na amani, tutawashughulikia na askari wameshajipanga na wana vifaa vya kisasa, atakayefanya fyoko tutamshughulikia kikamilifu.”Maandamano “Kuna wale wanaopenda kuandamana na mawe yanarushwa, nashangaa wanaosemaga polisi wanatumia nguvu kubwa huwa siwaelewi, semeni tunatumia nguvu ya kadri, mnapoandamana bila kibali ni makosa, maana yanakuwa sio ya amani, ni maandamano mabaya.“Niwasisitize tu, wakati wa uchaguzi mtu asithubutu kuandamana, nitakushughulikia pale pale, kama ni suruali yako itachanikia pale pale kabla hujafika mbali na kwenda kuleta madhara kwa watu wasio na hatia,” alisisitiza.Fitna, chuki majunguIGP Sirro alisema ili jeshi lifanye kazi vizuri, lazima wawe kitu kimoja, kwani kukiwa na chuki na majungu, kazi haziwezi kwenda vizuri.“Sitoi nafasi kwa mtu au kikundi cha watu kuwa na chuki na majungu, kazi yetu kama jeshi inahitaji upendo ili mambo yaende, mimi ni kiongozi na watu ninaowaongoza ni wengi, najua sio mkamilifu na siwezi kupendwa na watu wote.“Nilipoongea pale Bwalo la Polisi nilikuwa natoa angalizo, hata nilipomtaja RPC wa Kinondoni, sikumanisha yeye ndio analeta majungu, nilipitisha tu ujumbe kwake.“Kuna watu wana tabia za majungu majungu, ndio nilikuwa nawapa tahadhari na kuwakumbusha kaulimbiu yetu; ‘Umoja wetu ndio Nguvu yetu. Kama hatuna umoja na upendo, kazi itakuwa ngumu.Akijibu swali kuwa kupitisha ujumbe kwa mwingine ndio majungu kwa nini asiwe wazi, IGP Sirro alisema, “Mimi ni kiongozi, na kiongozi lazima uongee kwa mifano, pale nilikuwa natoa mifano tu, jeshi letu tunapendana sana.” Ajigamba anatoshau-IGP “Ninapojitathmini naona natosha tena sana, kama wapo wanaodai sitoshi ni kwa chini chini tu, lakini kazi yetu hatufanyi ndani ya chumba, hatujifungii ukiteuliwa IGP hujapitia vitengo vyote ndio utaambiwa hutoshi.“Lakini mimi nimepita sehemu mbali mbali kabla ya kuteuliwa IGP, binafsinajiona natosha sana, kama kuna binadamu wachache wanafikiria hivyo, nawaambia tu mimi nipo vizuri na naamini Watanzania wanajua,” anasema Sirro aliyeteuliwa kushika wadhifa huo Mei 28, 2017 akimbadili Ernest Mangu, ambaye ilielezwa kuwa atapangiwa kazi nyingine.Mangu sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Rwanda. Kabla ya uteuzi wa kuwa IGP, Sirro alikuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam akiwa na cheo cha Kamishna wa Polisi.Asema amedhibiti ujambazi, mauaji, ajali “Nilipoingia ujambazi ulikuwa juu hasa kwenye mitandao ya simu, na uvamizi wa vituo vya polisi na kutekwa silaha na watu kuuawa lakini matukio hayo yamepungua.“Changamoto nyingine niliyokutana nayo ni watu wa Kibiti, watu walikuwa wanakufa sana, lakini sasa Kibiti hata viwanja vimepanda bei, naona kuna kitu kimefanyika. “Sasa jeshi letu si legelege na kila mtu anaona umoja wetu ndio nguvu yetu na umoja ndio umetusaidia.“Ajali barabarani tumepunguza asilimia 47, haya ni mafanikio, lakini bado tunaendelea kupambana kuhakikisha tunazipunguza kwa asilimia ndogo zaidi.“Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo nikijitathmini naona natosha kwa asilimia zote, ingawa watu wa nje ndio wataweza kunitathmini vizuri zaidi,” alisema IGP.Amwita nyumbani Tundu Lissu Akizungumzia suala la aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) ambaye anaishi ughaibuni kwa sasa tangu alipojeruhiwa kwa risasi jijini Dodoma mwaka 2017, IGP Sirro alisema Jeshi la Polisi linafahamika kazi zake ni kulinda watu na mali zao, hivyo Lissu ni Mtanzania na akishakuja ni wajibu wao kama Jeshi la Polisi, kumlinda na kuhakikisha anakuwa salama.“Lissu na dereva wake tunawahakikisha usalama watakaporejea nchini, na pia itakuwa vizuri tukapata maelezo yao ya kina kwa aliyotendewa Lissu. Bila kupata maelezo kwa kina tunashindwa kupata mahali pa kuanzia, na pia dereva wake bila kumhoji kwa kina tunashindwa kupata pa kuanzia.“Kesi yoyote ya jinai inahitaji ushirikiano, kama hatujapata tutaanzia wapi?” alihoji.Aliongeza, “Bahati nzuri kesi ya jinai huwa haifi, siku akirudi na bahati nzuri ameshakuwa mzima na anatembea, naamini atatusaidia na tutapata majibu, na haki itatendeka.”Kigoma kinara wa uhalifu IGP Sirro alisema operesheni ambayo rais aliagiza ifanyike kukabiliana na uhalifu hasa kambi za wakimbizi, imezaa matunda kwani usiku wa kuamkia Oktoba 31, mwaka huu kwenye misitu ya Biharamulo waliua majambazi wanne, na kupata silaha aina ya AK47 na risasi nane.Alisisitiza kuwa operesheni inaendelea Kagera na Kigoma.Alisema Mkoa wa Kigoma bado unasumbua kwa uhalifu, hasa wa kutumia silaha sababu ya kambi za wakimbizi, ingawa alieleza kuwa matukio yamepungua kwa asilimia kadhaa, ukilinganisha na siku za nyuma ambako yalikuwa mengi.Hata hivyo, alisema lazima waongeze nguvu, na tayari wamepeleka askari wa kutosha na wanaendelea kufanya hivyo. Matukio ya ubakaji IGP Sirro alisema matukio ya ubakaji na kulawiti, yamekithiri na ndiyo yanayoshika kasi sana kwa sasa nchini.Alisema hiyo inatokana na uelewa wa watu, kwani wakifanyiwa vitendo hivyo wanaripoti polisi, tofauti na siku za nyuma ambako watu walikuwa wanaona aibu.Matukio ya ubakaji yameongezeka Tanzania katika kipindi cha Desemba 2015 kutoka 394 hadi kufikia 2,984 kwa Desemba 2017 ambalo ni ongezeko la matukio 2,590.Alisema jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wadau wengine, limechukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na ukatili dhidi ya watoto ikiwemo kuanzishwa kwa kamati za 10,988 ulinzi wa wanawake na watoto, na vikundi vya malezi 1,184 ikiwa ni pamoja na kuweka madawati ya jinsia kwenye vituo vya Polisi.“Pamoja na adhabu kali ambazo zimekuwa zikitolewa ingefaa watu waogope kujihusisha na vitendo vya ubakaji na ulawiti, lakini vitendo hivyo vimeendelea kuongezeka,” alisema Sirro.Kwa mujibu wake, wanaofanya matukio hayo wengi huwa wanatoka karibu na familia au ni ndugu wa watoto.Alisema uhalifu mwingine uliongezeka ni mauaji yanayotokana na ulevi, na mapenzi, “Viongozi wa dini watusaidie kama unamkuta mwanamke wako anaenda na mwanamume mwingine ni bora kuachana naye sio kumuua, ni mauaji ambayo Jeshi la Polisi peke yake haliwezi, viongozi wa dini, wanasiasa watusaidie,” alisema.Takwimu za Jeshi la Polisi za mwaka 2016 hadi Mei 2018 zinaonesha wanandoa 341 wameua wenza wao.Mikoa ya Geita, Singida, Mbeya, Mwanza, Tabora, Kagera, Songwe, Dodoma na Njombe, ndio iliyongoza kwa wanaume kuua wake zao wakati kwa upande wa wanawake kuua waume zao katika kipindi hicho mikoa iliyoongoza ni Tabora, Shinyanga, Kagera, Mwanza na Singida.Uvamizi benkiSirro anasema uvamizi na kuvunja kwenye mabenki umeisha, na hiyo inatokana na Jeshi la Polisi kuimarishwa zaidi pamoja na kushirikiana na wadau wengine wa ulinzi na usalama, wananchi pia wamekuwa wakitoa taarifa nyingi.“Wengi tumewakamata na wengine wametangulia mbele za haki wakati wa kuwakamata,na imefanikuwa kutokana na ushirikiano wa wananchi wamekuwa wakitupa taarifa nyingi sana za uhalifu,” alisema.Wizi wa mtandaoni Alisema uhalifu wa mitandao bado unasumbua kwani ni makosa ambayo ni mageni, na makosa yake yanavuka mipaka.Anasema ndio maana wamewapeleka askari nje ya nchi kupata mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na watu wa Interpol, ambao wanakuja kuwapa mafunzo maalumu. Azory yupo?Akijibu swali kuhusu alipo mwandishi huyo aliyekuwa akiripoti kutoka Rufiji mkoani Pwani, IGP Sirro alisema “Ni suala gumu kusema yupo au hayupo, maana tunasema ametekwa, nani aliyemteka, au ameenda kusaka maisha yake. Kama kuna mtu ana ushahidi atupe, jalada tumeshafungua.“Sina jibu moja kwa moja, tupo tayari kupokea ushahidi wowote kusaidia jambo lolote,” alifafanua IGP Sirro.-
3
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa mara ya kwanza imeandaa tuzo za kuwatambua watoa huduma za mawasiliano nchini zitakazofanyika Mei 17, mwaka huu huku ikisisitiza ni lazima kwa kila mwenye leseni yao kushiriki. Tuzo hizo zinajumuisha makundi 15 ikiwemo mtoaji huduma bora za simu wa mwaka, mtoaji huduma bora za mtandao wa mwaka, Televisheni bora ya Kitaifa ya mwaka, Televisheni bora ya Wilaya, Televisheni Mtandaoni, Blogger na watoa huduma za usafirishaji mizigo na vifurushi kitaifa na Kimataifa. Akitangaza tuzo hizo jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa TCRA, James Kilaba alisema lengo la kuandaa tuzo hizo ni kuwatambua watoa huduma wao na kuchochea utoaji wa huduma bora za mawasiliano nchini. Alisema ni lazima kwa kila mtoaji huduma ambaye amepata leseni ya TCRA kushiriki katika tuzo hizo na kwamba kwa kutokufanya hivyo ni kukataa leseni hiyo.“Utaratibu wa uandaaji wa tuzo hizi ulianza Julai mwaka jana lengo ni kila kada yenye leseni waweze kushiriki ili kujipima nafasi yao katika kutoa huduma,” alisema Kilaba na kuongeza pia malengo mengine ya kuandaa tuzo hizo ni kuboresha utoaji wa huduma na kwamba wateja watapata fursa ya kupiga kura kwa mtoa huduma wake ili kuongeza alama katika mchakato huo. Alieleza kuwa Mei 17 ya kila mwaka ni Siku ya Mawasiliano na Habari duniani na kwamba wamekuwa wakiyaadhimisha kwa matukio mbalimbali hivyo, waliona umuhimu wa kuweka tuzo hizo ili kutambua michango ya watoa huduma wote Tanzania. Mkurugenzi wa Idara ya Tehama na Huduma TCRA, Connie Francis alisema tuzo hizo zinahusisha makundi 15 ambazo ni mtoaji huduma bora za simu wa mwaka, mtoaji huduma bora za mtandao, televisheni bora ya Kitaifa ya mwaka, televisheni bora ya wilaya, redio bora ya kitaifa ya mwaka, redio ya mkoa, wilaya na ya jamii, televisheni mtandaoni, blogger na watoa huduma za usafirishaji mizigo na vifurushi.Francis alisema wataanza kupokea maombi kwa njia ya mtandao za kushiriki kwenye tuzo hizo kuanzia leo hadi Machi 15, mwaka huu ambapo watazipitia na kuchagua maombi yaliyowasilishwa.“Maombi haya yatumwe kwa http://ictawards.tcra.go.tz. baada ya kuyapitia maombi tutafungua dirisha la kupiga kura ambapo wateja wenu watapata nafasi ya kuwapigia kura kwa njia ya mtandao kuanzia Aprili Mosi hadi 30, mwaka huu pamoja na kutuma ujumbe wa maandishi kwenda namba 15072,” alisema Francis na pia baada ya upigaji kura watachagua washindi ndipo kutoa tuzo hizo.
3
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Wakili wa kujitegemea, Fatma Karume amejitosa kumrithi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa kugombea urais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), utakaofanyika Aprili 14, mwaka huu. Lissu, ambaye aliteuliwa kugombea nafasi hiyo lakini ameshindwa kukidhi matakwa ya kamati kutokana na fomu ya uteuzi iliyowasilishwa kwa sekretarieti hiyo. Kwa mujibu wa sheria mpya, Lissu hataweza kugombea tena nafasi hiyo kwani kifungu cha nane cha sheria hiyo, kinamzuia mtu ambaye ni kiongozi wa chama chochote  cha siasa, kuongoza chama hicho. Katika kinyang’anyiro hicho, Fatma atachuana na Godwin Mwapongo, Godfrey Wasonga na Godwin Ngwilimi huku nafasi ya umakamu wa rais ikiwa na mgombea pekee, Rugemeleza Nshalla na Mweka Hazina akiwa Sadock Magai. Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi wa chama hicho, Dk. Kibuta Ongwamuhana, uchaguzi wa rais utatanguliwa na viongozi wa kanda utakaofanyika kila mkoa kuanzia Machi 27, mwaka huu. Wakizungumzia uchaguzi huo baadhi ya mawakili wamesema wanamtabiria Fatma ushindi wa ishindo kutokana na kuwa na kariba inayofanana na Lissu. “Fatma atashinda kwa sababu anapenda mtu mwenye ‘tension’ na ni mtu mwenye kujiamini anaweza akaitetemesha serikali na wanasheria wanapenda hivyo,” amesema mawakili wa kujitegemea ambaye hakutaka jina lake litajwe. Wakili mwingine alisema ingawa sheria hiyo inamkataza Lissu kugombea ambapo walipanga kumchagua tena mwaka huu lakini Fatma anaweza kuziba pengo la Lissu.
3
WASHINGTON DC, MAREKANI MWANDISHI mkongwe nchini hapa na rais wa zamani wa Kampuni ya vichekesho ya  Marvel Comics,  Stan Lee, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 95. Mwaka 1961, Lee alibuni filamu nne bora za Marvel Comics na kuzipatia majina maarufu ikiwemo Spider-Man na The Incredible Hulk. Kwa mujibu wa wakili wa familia yake, mwandishi huyo mkongwe wa vitabu vya vichekesho alifariki dunia katika kituo cha matibabu cha Cedars Sinai kilichopo mjini Los Angeles. Ofisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya burudani ya Pow inayomilikiwa na Lee, alimtaja kama baba wa mitindo ya pop kwa kubuni wahusika wanaofahamika kote duniani. Mkurugenzi Mkuu Shane Duffy alimkumbuka kama mwanzilishi wa kweli ambaye hana mpinzani. Akizungumza na mtandao wa TMZ unaoangazia habari za watu mashuhuri, binti yake, JC Lee alisema baba yake alikuwa mtu mashuhuri na mwenye heshima. Binti huyo pia aliliambia Shirika la Habari la Uingereza – Reuters kwamba katika utendaji kazi wake alihisi kuwa na wajibu mkubwa kwa watu. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Marekani, miaka ya hivi karibuni, Lee amekuwa akiiugua mara kwa mara. Lee alifahamika kwa kutengeneza filamu maarufu alipokuwa na kampuni ya filamu ya Marvel, japo aliachana na kampuni hiyo mwaka 1972. Siku ya Jumapili, ambayo ni siku ya kuwatambua mashujaa, ukurasa wake rasmi wa Facebook uliweka picha zake akiwa jeshini, na kuandika kwa utani kwamba alikuwa mtunzi wa michezo tangu wakati wa vita ya pili ya dunia.
2
Derick Milton -Simiyu  UONGOZI wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Simiyu, umesema kasi kubwa ya wananchi wanaojitokeza kupima na kupatiwa chanjo ya ugonjwa wa homa ya ini, imesababisha kuwapo uhaba wa chanjo hiyo. Kutokana na changamoto hiyo, hospitali hiyo inalazimika kutoa chanjo kwa vipindi kwani mahitaji ni makubwa kuliko uwezo wake wa kununua chanjo hiyo kutokana na uchanga wake. Akizungumza na waandshi wa habari hospitalini hapo jana, mtaalamu wa maabara, Raphael Kambona alisema wanakutana na tatizo la upatikanaji wa chanjo ya homa ya ini za kutosha hali inayowalazimu kusitisha huduma hiyo kwa vipindi. Kambona alisema ndani ya miezi sita tangu hospitali hiyo ianze kutoa huduma, mwitikio wa wananchi wa kupima na kupatiwa chanjo umekuwa mkubwa sana na wamefikia hatua ya kusitisha kupokea wateja wapya. “Kuna wakati tunalazimika kusitisha kupokea wateja wapya kuwapatia chanjo, akiba tuliyonayo ni kidogo na endapo tutawaanzishia chanjo wateja wapya, tutashindwa kuwakamilishia dozi wateja wa zamani. “Tumekuwa tukiwarudisha wateja wetu wapya kwa sababu ya uhaba wa chanjo, na tunafanya hivyo ili wale waliokwisha anza waweze kupata kwa mtiririko unaotakiwa na tukishawaanzishia ni lazima tuwakamilishie dozi kwa  awamu tatu,” alisema Kambona. Alisema mwitiko wa wananchi kuwa mkubwa unatokana na wengi wao kutangaziwa mara kwa mara kuhusu madhara ya ugonjwa huo na umuhimu wa kupata chanjo. Kambona alisema ndani ya miezi sita, wananchi 251 sawa na asilimia 3.2 walijitokeza kupata huduma ya upimaji na chanjo ya homa ya ini na kati ya hao wanane waligundulika na homa hiyo na kupewa rufaa za kwenda Hospitali ya Bugando kwa matibabu zaidi. Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk. Matoke Mayenjwa alisema tatizo kubwa la changamoto hiyo ni uwezo wa kifedha wa hospitali unaotokana na uchanga toka imeanza kufanya kazi. Lakini alieleza kuwa kadiri wanavyoendelea kufanya kazi, ndivyo watakavyoweza kujitosheleza kwa kila kitu. “Uchanga ndiyo tatizo, bado hatujaweza kujitosheleza kibajeti, ila ni matumaini yetu tukiendelea kufanya kazi vizuri tutaboresha huduma muhimu ambazo kwa sasa bado hazijakamilika ipasavyo,” alisema Dk. Matoke. Hospitali hiyo ilizinduliwa Septemba 2018 na Rais Dk. John Magufuli na ilianza kutoa huduma mbalimbali Juni, mwaka jana.
0
    Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM INAWEZEKANA wewe ni miongoni mwa watu wanaopenda kuongeza chumvi kwenye chakula pindi kinapokuwa kimetayarishwa mezani tayari kwa kuliwa. Watu wengi hasa walaji wa nyama choma na chipsi hupendelea kuongeza chumvi mezani kwa madai kwamba chakula hakijakolea ladha ile wanayoihitaji. Wataalamu wanaeleza kuwa chumvi ni kiungo muhimu katika chakula kwani licha ya kuongeza ladha ina ‘utajiri’ mkubwa wa madini ya sodium chloride ambayo huhitajika mno mwilini. Wanataja faida za chumvi kuwa ni pamoja na kuweka sawa hali ya maji mwilini (fluid balance), husaidia katika kuweka sawa mtiririko wa mapigo ya moyo (heart rhythm) pia husaidia katika kutanuka na kusinyaa kwa kisuli (contract and relaxation of muscles). Lakini wanasema ili mtu apate faida hizo ndani ya mwili wake chumvi inapaswa kupikwa jikoni na kuiva pamoja na chakula na si kuongeza mezani. Wanasema kitendo cha kuongeza chumvi mezani (mbichi) ni cha hatari na kwamba husababisha mtu kupata magonjwa mbalimbali hasa shinikizo la juu la damu katika maisha yake. Anasema uwezekano wa mtu kupata shinikizo la juu la damu kutokana na ulaji mbovu wa vyakula hasa vilivyoandaliwa kwa kutumia mafuta mengi ni mkubwa. “Chipsi hupikwa kwa kutumia mafuta mengi na kawaida watu wanapokula huweka chumvi nyingi pamoja na wale wanaokula nyama choma hutumia chumvi nyingi, ulaji huo si mzuri na si salama kiafya. Anasema tafiti zinaonesha watu weusi (Waafrika) tunapenda zaidi kutumia chumvi nyingi tofauti na watu wa mabara mengine. “Mbaya zaidi inaonekana miili yetu ina inapokea haraka mno ile chumvi inayoingia mwilini ikilinganishwa na wenzetu weupe, hivyo kutusababishia madhara,” anasema. Anasema mtindo wa maisha wa sasa unachangia kwa kiwango kikubwa watu kupata magonjwa ya moyo kuliko mtindo wa maisha wa kale. “Wengi leo hii hatufanyi mazoezi, muda mwingi tunakaa maofisini, tunatumia usafiri wa bodaboda na magari kutoka sehemu moja kwenda nyingine, matumizi ya sigara na pombe ni ya kiwango kikubwa na ulaji wetu si mzuri kwa ujumla, mambo haya yanachochea kuongezeka kwa magonjwa ya moyo hasa shinikizo la juu la damu,” anasema. Wengi hufa kimya kimya Anasema hivi sasa ulimwenguni magonjwa ya moyo ndiyo yanayongoza kusababisha vifo vya watu wengi. “Wakati mwingine mtu anaweza asigundue kama shinikizo lake la damu lipo juu, inawezekana kabisa asione hata dalili yoyote, haumwi kichwa wala miguu,” anasema. Anaongeza; “Wengi huja hospitalini wakiwa tayari moyo haufanyi kazi sawa sawa au figo zimeharibika, tunapowapima tunagundua kuwa wana shinikizo la juu la damu, ndiyo maana ugonjwa huu unaitwa ‘silent killer’ kwa sababu unakula taratibu ndani ya mwili wako. Tafiti Daktari huyo anasema tafiti zinaonesha kuwa zaidi ya theluthi moja ya vifo vyote duniani hutokana na magonjwa yanayohusishwa moja kwa moja na moyo. Anasema kati ya hiyo theluthi moja magonjwa ya moyo zaidi ya asilimia 50 yanatokana na shinikizo la juu la damu (hypertension). “Katika miaka ya nyuma tatizo lilikuwa zaidi katika nchi zilizoendelea lakini katika miaka ya hivi karibuni kulingana na tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika inaonekana tatizo lipo zaidi katika nchi zinazoendelea. Anasema inaonekana shinikizo la juu damu ni namba moja kwa kusababisha magonjwa ya moyo katika nchi zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara, Tanzania ikiwamo. “Tafiti moja kubwa iliyofanywa katika nchi 23 barani Afrika ilionesha katika nchi zote hizo, shinikizo la damu linashika namba moja kwa kusababisha moyo kushindwa kufanya kazi na vifo vya ghafla,” anasema. Anasema katika nchi hizo zilizofanyiwa utafiti huo (Tanzania ikiwamo) ilionekana asilimia 86 ya magonjwa yote ya moyo hutokana na shinikizo la damu. Hali ilivyo JKCI Daktari huyo ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Utafiti na Mafunzo wa JKCI anasema tafiti zilizofanywa na taasisi hizo zinaonesha tatizo ni kubwa katika jamii. “JKCI tumewahi kufanya tafiti miaka mitatu iliyopita, ambazo zilihusisha jamii moja kwa moja na wagonjwa waliolazwa wodini, tumebaini tatizo ni kubwa. “Kwenye tafiti zilizohusisha jamii asilimia kati ya 42 hadi 56 ya watu tuliowapima walikuwa na shinikizo la juu la damu,” anasema. Anaongeza; “Asilimia 35 hadi 47 ya wagonjwa waliokuwa wamelazwa wodini ambao mioyo yao ilikuwa ime-fail (imeshindwa kusukuma damu sawa sawa), tulibaini kisababishi kikuu ni shinikizo la juu la damu. Vijana hatarini Anasema wakati katika nchi zilizoendelea tatizo hilo likijulikana kama ni ugonjwa wa watu wazima hali ni tofauti katika nchi zinazoendelea kwani linawakumba zaidi vijana. “Katika nchi zilizoendelea watu wanaokutwa na shinikizo la juu la damu ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 50 na kuendelea, lakini katika nchi zinazoendelea hasa kusini mwa jangwa la sahara wanaokutwa na tatizo hilo ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 35 hadi 45, ambao kimsingi ni umri wa uzalishaji,” anasema. Je, watoto nao wanaugua Anasema watoto nao hupata shinikizo la juu damu lakini mara nyingi hali hiyo hutokea iwapo wamepata maradhi mbalimbali ikiwamo saratani. “Tatizo hili limegawanywa katika makundi mawili kuna ‘primary hypertension’ na ‘secondary hypertension’. Tunaposema ‘secondary hypertension tunamaanisha kwamba kunakuwa na kisababishi kingine ambacho kinasababisha mtu kupata shinikizo la juu la damu. “Kwa mfano saratani au mvurugiko wa homoni kwenye damu na mara nyingi hii ndiyo ambayo huwakumba watoto na kusababisha kupata shinikizo la juu la damu,” anasema na kuongeza: “Lakini tunaposema ‘primary hypertension’ mara nyingi huwakumba zaidi watu wazima, yaani hapa tunampima mgonjwa lakini tunakuta hakuna tatizo lolote ambalo limesababisha wao kupata shinikizo la juu la damu. Asilimia 95 ya pressure zote ni primary hypertension.” Anasema hata hivyo watoto ni nadra mno kupata tatizo hilo na kwamba kwa mwaka huwa wanawapokea watoto watano wenye shinikizo la juu la damu ikilinganishwa na watu wazima 400 hadi 500 ambao hufika katika taasisi hiyo wakisumbuliwa na shinikizo la juu la damu. Matibabu Anasema si rahisi kutibu shinikizo la juu la damu kwani mgonjwa hulazimika kutumia dawa siku zote za maisha yake tangu anapogundulika kuwa na tatizo hilo. “Matibabu ya shinikizo la damu pamoja na kuwa yanajulikana na dawa zimethibitishwa kisayansi lakini ni miongoni mwa magonjwa ambayo hayatibiwi kisahihi, hii ni changamoto,” anasema. Anasema changamoto hiyo ipo zaidi katika nchi zinazoendelea ambapo tafiti zinaonesha asilimia 18 ya watu wenye tatizo hilo katika nchi zinazoendelea ndiyo ambao hutumia dawa ikilinganishwa na asilimia 87 katika nchi zilizoendelea. “Na katika hao asilimia 18 waliopo kwenye dawa ni asilimia sita tu ndiyo ambao wameweza ku-contral pressure zao, hawa wanazingatia matibabu yao. “Katika nchi zilizoendelea watu hugundulika mapema na kuanza tiba lakini nchi zinazoendelea ni tofauti wengi huja hali ikiwa mbaya, hivyo kuna mambo mawili hapa, moja ni watu kuchelewa hospitalini na watu kutozingatia matibabu na masharti ya chakula wanayopewa na watalaamu,” anasema. Wengi hawamudu gharama Daktari huyo anasema gharama za kutibu tatizo hilo ni kubwa iwapo mtu hana bima yoyote. “Nimesema awali kwamba mtu mwenye ugonjwa huu analazimika kumeza dawa kila siku tangu alipokutwa na tatizo, kwa kuwa matibabu ni ghali, changamoto tunayoona ni baadhi ya wagonjwa wetu ambao hawana bima wanafika mahali wanashindwa kugharimia matibabu yao,” anasema. Anasema matibabu yenyewe hutegemeana na idadi ya dawa ambazo mgonjwa huandikiwa kulingana na kiwango cha shinikizo la damu alichonacho. “Mgonjwa hupewa dawa kulingana na kiwango cha ‘presha yake, kuna ambao hutakiwa kutumia kidonge kimoja au viwili kwa siku, ikiwa juu hulazimika kutumia vidonge vitatu, vinne au hata vitano kwa siku ili kuiweka sawa. “Sasa unaweza kukuta kidonge kimoja ni Sh 200 na kama hicho hakimsaidii anaweza kuandikiwa kidonge kimoja cha Sh 1,000, akitakiwa kumeza hicho cha Sh 200 kwa siku maana yake anahitaji kuwa na Sh 60,000 kwa mwezi apate dozi kamili, wengi wanashindwa kumudu gharama hizo,” anasema. Anasema kutokana na hali hiyo wanakuwa hawatumii dozi kama inavyopaswa jambo ambalo ni la hatari. “Kwa kawaida hakuna kikomo cha matumizi ya dawa, huu ni ugonjwa wa kudumu, kila siku mtu anapaswa kutumia dawa ingawa anaweza kufika mahali akapunguziwa dozi na daktari wake iwapo presha yake inakuwa imeshuka na hapo ndipo zile gharama za matibabu nazo zinapungua,” anafafanua. Elimu ni ndogo Daktari huyo anasema jamii bado haina uwelewa wa kutosha juu ya tatizo hilo. “Wengi hawana mwamko wa kuchunguza afya zao, ndiyo maana wanaletwa hospitalini wakiwa shinikizo la damu limefika 200 na zaidi na tayari wamepata madhara makubwa,” anasema. Madhara Anasema wapo ambao hufikishwa hospitalini macho yakiwa hayaoni, moyo hausukumi damu sawa sawa, wana kiharusi au figo hazifanyi kazi sawa sawa. “Na wale wanaokuwa hawatumii dawa inavyotakiwa wapo kwenye hatari ya kupata madhara haya katika siku za usoni,” anabainisha. Kuhusu shinikizo la chini la damu Daktari huyo anasema tatizo hili haliwapati watu wengi ikilinganishwa na shinikizo la juu la damu. “Kwa mwezi hapa JKCI tunaweza kupokea watu 10 wanaosumbuliwa na shinikizo la chini la damu kuliko wale wenye shinikizo la juu ambao wanaweza kufikia zaidi ya 200, watu wenye shinikizo la chini la damu matibabu yao ni rahisi mara nyingi wakitundikiwa dripu ya maji hurejea katika hali ya kawaida,” anasema. Kuhusu maadhimisho Anasema kutokana na hali hiyo, Shirika la Afya Duniani (WHO) ilichagua Mei 17, kila mwaka kuwa Siku ya Mapigo ya Moyo Duniani. “WHO ilitenga siku hii ili kuelimisha jamii kuhusu madhara ya shinikizo la damu na watu wapate fursa ya kuchunguza afya zao ili wale wanaogundulika waanze kupata matibabu mapema,” anasema.
0
Wenyeji wa Fanali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2019 (Afcon), Misri ambao ni mabingwa mara saba wameanza michuano hiyo kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Zimbabwe katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Cairo. Mechi hiyo ya ufunguzi wa michuano ya Afcon kwenye Uwanja wa Taifa jijini Cairo, Misri walikwenda mapumziko kwa uongozi wa bao 1-0, mfungaji akiwa Mahmoud Hassan ‘Trezeguet’.   Khama Billiat anayekipiga Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini ndiye alikuwa ndiye alikuwa msumbufu zaidi kwa upande wa Zimbabwe dhidi ya Mafarao hao lakini ngome ya Misri ilisimama imara kwa kuondoa hatari zote zilizokuwa zikielezwa goli kwao. Zimbabwe walionekana kucheza kwa kujiamini lakini tatizo likawa ni mashambulizi dhaifu ambayo ama yaliishia kwa kipa au kutoka nje. Trezeguet, alifunga goli hilo akiwa na mpira baada ya kupiga shuti kutokea umbali wa takriban mita 30 akitokea pembeni mnamo dakika ya 41 na kuipa uongozi timu yake. Kipindi cha pili kilitawaliwa na mashambuliz ya zamu kutoka timu zote mbili lakini kwa upande wa Misri, nyota wa Liverpool Mohamed Salah hakuwa na mchezomzuri kutokana na kukosa nafasi kadhaa za wazi. Michezo ya Kundi A itaendelea tena Jumatano ambapo Misri watacheza dhidi ya Timu ya Taifa ya DR Congo huku Zimbabwe wakiwakabili Uganda, timu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki. Kikosi cha Zimbabwe Kilichoanza: Tedmore Sibanda, Tendayi Darikwa, Devine Lunga, Alex Mudimu, Teenage Hadebe, Marshall Munetsi Marvellous Nakamba, Obvious Karuru, Knowledge Musona, Khama Billiat, Nyasha Mushewa Benchi: Danny Phiri, Ronald Pfumbidzai, Talent Chawapiwa, Evans Rusike, Jimmy Dzingai, Elvis Chipezeze, Tino Kadewere, George Chigova, Knox Mutizwa,Nabil Dunga Thabani Kamusoko, Tafadzwa Kutinyu Kikosi cha Misri kilichoana: Ahmed El Shenawy(Kipa), Ahmed El Mohanady, Mahmoud Alaa El-Din, Ahmed Hegazy, Ayman  Ashraf, Tarek Hamed, Mohamed Elneny, Mohamed Salah, Amr Warda, Trezeguet, Marwan Mohen. Benchi: Mahmoud Genish‏(Kipa), Baher Elmohamady, Omar Gaber, Ahmed Mansour,Mahmoud Hamdy, Ali Ghazal, Walid Soliman, Nabil Emad, Ahmed Ali, Ahmed Hassan
4
ROME, ITALIA MAMILIONI  ya watu barani Ulaya wanaanza kurudi kwenye maisha ya kawaida, baada ya wiki kadhaa za kujifungia ndani kwa hofu ya maambukizo ya virusi vya korona lakini wanakaribishwa na dunia ambayo si kama walivyoiwacha. Anga la rangi ya bluu linawakaribisha wakazi wa Mji Mkuu wa Italia, Rome, katika dunia ambayo kamwe haitakuwa tena ile waliyoiwacha wiki kadhaa nyuma wakati walipolazimika kujifungia ndani kwa hofu za maambukizo ya virusi vya Corona. Kuna mengi yaliyobadilika na ambayo huenda yasirejee tena kwenye hali ya zamani. Italia, taifa la pili baada ya Marekani kwa kuwa na vifo vingi vya wagonjwa wa Covid-19, limeanza rasmi shughuli za uzalishaji mali jana, Jumatatu Mei 4 kwa kufungua viwanda na maeneo ya ujenzi. Migahawa nayo imefunguliwa, lakini kwa huduma za kuchukua tu chakula, huku baa na maeneo mengine ya starehe yakiendelea kufungwa. Watu wanashauriwa kuepuka kutumia usafiri wa umma, na wachache wanaoutumia, wanalazimika kuvaa barakoa. Uchumi wa Italia, ambao ni wa tatu kwa ukubwa katika Ukanda wa Euro, unatazamiwa kusinyaa katika kiwango ambacho hakijawahi kutokea tangu mfadhaiko wa Kiuchumi wa Kilimwengu wa miaka ya 1930.  Kwa Marekani, taifa linaloongoza kwa maambukizo na vifo, inuko la kiuchumi lilikuwa liwe alama kuu ya mafanikio ya Donald Trump kwenye kampeni yake ya kuomba kuchaguliwa tena kuwa rais kwenye uchaguzi wa Novemba. Lakini wiki kadhaa za zuio la shughuli za maisha limepelekea Wamarekani milioni 30 kupoteza ajira zao, na sasa kiwango cha uungwaji mkono kwa Trump kimeshuka.  Mwenyewe Trump aliongeza mashambulizi yake dhidi ya China, akiituhumu kuwa chanzo cha kirusi ambacho anasema kilianzia kwenye maabara moja mjini Wuhan. Kauli hiyo sasa inaungwa mkono na waziri wake wa masuala ya kigeni, Mike Pompeo, ambaye alisema ana ushahidi wa kutosha kuwa virusi vya corona ni zao la maabara za Kichina. “Nadhani dunia nzima inaweza kuona sasa, na kumbuka, China ina historia ya kuuambukiza ulimwengu na kuendesha maabara zilizo chini ya viwango,” alisema Pompeo siku ya Jumapili bila kutaja hasa kilipo chanzo cha ushahidi wake. Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa Marekani alisema kuwa bado wachambuzi wanachambua taarifa walizokusanya kujuwa asili hasa ya virusi hivyo. China, kwa upande wake, inakanusha madai hayo. Hadi sasa wanasayansi wengi wanakubaliana kuwa ugonjwa wa Covid-19 ulitokana na jamii ya wanyama kwenda kwa wanadamu kwa utaratibu wa kawaida wa kimaumbile. Kurejea kwa kauli hizi dhidi ya China kutoka Serikali ya Marekani kumeyatikisa masoko ya hisa, huku wawekezaji wakiwa na wasiwasi endapo zinaweza kuishia kwenye vita vya kibiashara kati ya mataifa hayo makubwa duniani. Soko kuu la hisa la Hong Kong limeshuka kwa asilimia nne, huku mengine barani Asia yakipoteza asimilia mbili na ya Ulaya yakianza Jumatatu hii kwenye mstari mwekundu. Kiasi cha watu 248,000 wamepoteza maisha yao tangu virusi vya corona kuibuka nchini China mwishoni mwa mwaka uliopita na haraka sana kikaweza kusambaa kwenye mataifa mengine na kuwaambukiza watu wapatao milioni tatu na nusu.
2
MILA potofu juu ya lishe katika baadhi ya makabila mkoani Singida, zimetajwa kuwa ni moja ya sababu ya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kukumbwa na utapiamlo kutokana na wazazi wao kutopata mlo kamili wakati wakiwa wajawazito na hata baada ya kujifungua.Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa habari hizi kwa jamii ya kabila la Wanyaturu, ambalo ndilo kabila kuu mkoani Singida, unaonesha kuwa licha ya elimu juu ya umuhimu wa lishe bora kwa wanawake wajawazito na anayenyonyesha kutolewa mara kwa mara, baadhi ya vyakula bado haviliwi na kundi hilo ili kutii matakwa ya kimila.Patrick Mdachi ambaye ni Ofisa Maendeleo ya Jamii mstaafu alisema kuwa hadi hivi sasa ni mwiko kwa mwanamke mjamzito wa kabila la Kinyaturu kula mayai kwa imani kuwa mtoto atakayezaliwa hataota nywele kichwani na anaweza kufa ghafla.Alisema vyakula vingine zinavyozuiwa na wazee wa mila ni pamoja na utumbo mwembamba kwa madai kuwa ndoa itayumba na maini kwa madai kuwa mtoto tumboni anatakuwa mnene na kuwa na uzito mkubwa, hivyo kusababisha upasuaji wakati wa kujifungua ambapo utumbo wa ‘daftari’ wa mbuzi au ng’ombe unaaminika kuleta mabaka kichwani kwa mtoto.“Mimi ni mtafiti wa masuala ya kimila na nimeandika kitabu maalum cha Wanyaturu wenzangu na mila zao, kwa hiyo najua vyema na orodha ni ndefu ya vyakula vinavyozuiwa kuliwa na wajazito lakini itoshe tu kusema kuwa bado tuna safari ndefu kupinga mila potofu za lishe bora,” alisema Mdachi.Baadhi ya wanawake wazee ambao hawakupenda kutajwa majina yao gazetini wanadai kuwa kuzuiwa kula baadhi ya vyakula ndiko kulikosababisha wanawake wengi kujifungulia nyumbani bila matatizo yoyote enzi hizo tofauti na hivi sasa kwani wengi wanaenda hospitalini na baadhi yao hujifungua kwa upasuaji huku matatizo yatokanayo na uzazi yakiwa lukuki..Hata hivyo, Ofisa lishe wa Mkoa wa Singida Teda Sinde alisema hoja za wanawake hao zinadhihirisha wazi kuwa bado kuna changamoto kubwa ya mila potofu juu ya masuala ya lishe katika baadhi ya makabila na kuchangia kuwepo kwa tatizo la utapiamlo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kutokana na mlo duni kwa baadhi ya wanawake wajawazito na waliojifungua.Alisema kuwa Ofisi yake imeona changamoto hiyo na kuanza kutoa elimu kwa jamii juu ya uandaaji wa lishe bora na kupiga vita mila potofu zinazozuia baadhi ya vyakula muhimu kiafya kwa sababu za kimila.Takwimu za utafiti wa kitaifa juu ya hali ya lishe mkoani Singida kwa mwaka juzi (TNNS 2018 ) zinaonesha kuwa asilimia 29.8 ya watoto chini ya miaka mitano wana tatizo la udumavu, asilimia tano ukondefu na asilimia 15 wana uzito mdogo wakati asilimia 27.9 tu ya watoto hao ndio walionyonyeshwa maziwa ya mama kwa kipindi cha miaka miwili.
3
WANANCHI wa Mkoa wa Pwani wametahadharishwa kujikinga na ugonjwa wa homa ya dengue ambao hadi sasa kuna wagonjwa 42 wanaougua ugonjwa huo. Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo kwenye kikao maalumu cha Kamati ya Ulinzi na Usalama na wadau mbali mbali wakiwemo Kamati ya Amani inayoundwa na viongozi wa madhehebu mbali mbali na viongozi wa afya na Wilaya ambazo zimeguswa na ugonjwa huo.Ndikilo alisema uwepo wa ugonjwa huo uliripotiwa Mei 8, mwaka huu, ambao mgonjwa wa kwanza alibainika wilayani Kibaha ambaye alitokea Msewe jijini Dar es Salaam. “Wilaya inayoongoza kuwa na wagonjwa wengi wa ugonjwa huu ni Mkuranga 35, Rufiji 4 na Kibaha 3 hali ambayo wananchi na wataalamu wa afya washirikiane ili kuuwa mbu na mazalia yao,” alisema Ndikilo.Alisema ili kukabiliana na ugonjwa huo viongozi wa dini wanapaswa kutoa elimu juu ya ugonjwa huu pia vipeperushi vya ugonjwa huo viwekwe kwenye mbao za matangazo, maofisini na sehemu zenye watu wengi. Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dk Gunini Kamba alisema ugonjwa huo unasambaa kwa kasi hivyo wananchi wachukue tahadhari.Kamba alisema vipimo kwenye vituo vya afya vya serikali gharama zake ni bure na kwa vile vya watu binafsi zisizidi Sh 15,000. Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama alitaka elimu itolewe sehemu mbali mbali hasa zile zenye mikusanyiko ya watu ili wapate uelewa juu ya ugonjwa. Mshama alisema yeye aliugua ugonjwa huo na kupatiwa matibabu, hivyo wananchi wanapaswa kuwa makini kujikinga kwa kuua mazalia ya mbu na kujikinga.Mkuu wa Wilaya ya Kibaha mstaafu, Halima Kihemba alisema kuwe na utaratibu wa uchafu unaokusanywa sehemu mbali mbali kutupwa sehemu husika ili kupunguza mazalia ya mbu. Homa ya dengue hutokana na mtu kuumwa na mbu aina ya Aedes mwenye virusi vya ugonjwa huo ambao unaweza kuhatarisha maisha ya watu. Umeenea katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Singida na Tanga.
3
Bethsheba Wambura, Dar es Salaam Rais John Magufuli, amezindua ghala kuu na mitambo ya gesi ya Kampuni ya Taifa Gas Ltd. inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz ambapo amewataka Watanzania wanaotumia mkaa kuanza kutumia gesi ili kupunguza gharama na kujilinda kiafya. Aidha, amezipongeza sekta binafsi kwa kuamua kuungana na serikali kuwekeza katika gesi asilia. “Nitoe wito kwa Watanzania ambao wamezoea kutumia mkaa waanze kutumia gesi kwa sababu kwanza wanapunguza gharama lakini pia wanajilinda kiafya kwani gesi ni salama na nafuu kutumia. “Lakini pia nimefurahi kuona mmiliki na wengine wanaomiliki kampuni hii kwa asilimia 100 ni wazawa, nikupongeze sana Rostam na Watanzania wengine kwa uwekezaji na kuweza kutoa ajira zaidi ya 200 kwa Watanzania,” amesema Rais Magufuli. Amesema ameambiwa kutokana na uwekezaji huo, kampuni hiyo imefanikiwa kulipa kodi hadi kufikia Sh bilioni moja, na kuwa matumaini yake kuwa kodi itaongezeka kadri uzalishaji wa gesi utakavyokuwa naendelea kuwapongeza ambapo ameahidi kuwa serikali iko pamoja nao. “Naomba Serikali iache kuingilia sekta binafsi walishindwa kuleta hii gesi hapa leo wameona iko tayari wanakimbia kimbia kufanya nini, lazima mambo haya tushirikiane ili yaende. “Kuna wakati fulami tuliwahi kuchukua uamuzi fulani mgumu, kulikuwa na kampuni inaitwa TIPA leo haipo naomba sana yasije kutokea kama yalivyotokea TIPA ikasambaratika,” amesema Rais Magufuli. Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati kuhakikisha gesi asilia inafika katika maeneo ambayo haijafika japo wizara yenyewe ina nishati yake asilia lakini ihakikishe na hii nyingine inafika katika maeneno mengi. “Lakini nawasihi na ninyi wasambazaji mpunguze bei ya mitungi, na nimefurahi kusikia kuwa  Taifa Gas mtatengeneza mitungi yenu wenyewe na hiii itafanya bei ya gesi ipungue na kila Mtanzania atamudu kununua,” amesema.
3
Akizungumza na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dk Reginald Mengi jana jijini Dar es Salaam, Yoshida alisema kwa kuwa kilimo ndicho kimeajiri watu wengi nchini na wanahitaji kupata masoko nje ya nchi ikiwemo Japan, yuko tayari kuzungumza na kampuni kadhaa ziweze kuingia ubia na Watanzania.Alitoa kauli hiyo baada ya Dk Mengi kumwomba balozi huyo kama inawezekana asaidie Watanzania kuingia ubia na kampuni za kijapan katika kusaidia kukuza uchumi wa Mtanzania wa kawaida ambaye kwa sasa licha ya uchumi wa nchi kukua lakini hajaona faida ya ukuaji wa uchumi huo.Dk Mengi alisema Mtanzania wa kawaida anataka kuona na yeye anafaidika na kukua kwa uchumi huo ambao umefikia asilimia 7 na akamuuliza balozi huyo ni namna gani anaweza kusaidia katika eneo hilo.Moja ya eneo ambalo alisema ni muhimu ili Watanzania waweze kukubalika kwenye masoko ya nje ya nchi ni kuboresha vifungashio vya mazao yao na akasema katika suala la kuuza nje ubora wa bidhaa pamoja na vifungashio ni jambo la msingi.Kwa upande wake Dk Mengi alisema kama Japan iko tayari kuwasaidia Watanzania ni vyema ikatoa fedha na kuipa Serikali ya Tanzania ili iweze kutoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo chini ya udhamini wa Serikali yenyewe.Wakati huo huo balozi huyo aliwataka Watanzania ambao wataenda kutembelea maonesho ya Sabasaba kwenda kwenye mabanda ya maonesho ya kampuni za kijapan ambako alisema moja ya maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ni suala la uuzaji wa bidhaa za umeme wa jua.“Kampuni za kijapani baadhi zipo hapa nchini na kwenye maonesho watakuwepo, hivyo nitoe wito kwa Watanzania ambao watapenda kuingia ubia na kampuni za kijapani waende kwenye mabanda yao watajionea maeneo ambayo wataona watashirikiana,” alisema.
5
KOCHA wa timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, Hemed Morocco amesema kuwa anakiamini kikosi chake kwa namna alivyokiona katika kuelekea kwenye michuano ya Cecafa Chalenji inayotarajia kuanza rasmi kesho Jumamosi.Michuano hiyo safari hii inafanyika mjini Kampala nchini Uganda huku bingwa mtetezi ikiwa ni Kenya iliyotwaa kombe hilo mwaka 2017 kwa kuifunga Zanzibar katika fainali iliyoisha kwa sare 2-2 kabla ya kuibuka kidedea kwa penalti 3-2.Morocco ameeleza kuwa kikosi chake ni kipana mno na kilikuwa na changamoto kubwa katika uteuzi wa wachezaji watakaoenda kuiwakilisha Zanzibar katika michuano hiyo. Pamoja na hayo, kocha huyo ameeleza kuwa kamili katika kila idara isipokuwa amekuwa na upungufu ambao ni wa muda mrefu katika nafasi ya beki wa kulia ingawa safari hii imeleta ahueni kutokana na kuwa na machaguo mengi katika nafasi hiyo.“Changamoto ya kutaja kikosi ilikuwa kubwa, kikosi ni kizuri kila mmoja anajitoa isipokuwa katika nafasi ya beki wa kulia tangu mwaka 2017 imekuwa ikisumbua japokuwa safari hii nilikuwa na machanguo matatu kabla ya kuwachukua wawili ambao kulingana na mfumo, wote walikuwa wanaonesha uwezo mkubwa.
4
SERIKALI imetoa kanuni mpya za usimamizi wa mazingira katika kutekeleza agizo la kutotumika kwa mifuko ya plastiki nchini ambapo faini zake zimo za kifungo cha siku saba jela na faini ya hadi Sh bilioni moja.Chini ya kanuni hizo mpya, atakayekutwa na mfuko wa plastiki atatozwa faini ya kati ya Sh 30,000 hadi Sh 200,000 pamoja na kifungo cha siku saba, huku msafirishaji wa mifuko hiyo nje ya nchi akikabiliwa na faini ya kati ya Sh milioni tano hadi Sh milioni 20 au kifungo cha miaka miwili jela.Hata hivyo wauzaji wadogowadogo watakaokutwa na mifuko hiyo faini yake ni Sh 100,000 hadi Sh 500,000 pamoja ama kifungo cha miezi mitatu jela.Pamoja na kanuni hizo, serikali imesisitiza kuwa asiwepo mtendaji au mgambo atakayehusika kupiga virungu, kubeba mtu yeyote kwa kosa la kukutwa akiwa amebeba mfuko wa aina hiyo badala yake elimu itawale ya kuzuia matumizi ya mifuko hiyo.Kadhalika kanuni hizo zimetoa mamlaka kwa serikali za mitaa, kutoza faini hizo na zibakie katika chombo hicho hadi hapo utaratibu mwingine utakapotolewa baadaye.Kanuni hizo zilisomwa Dar es Salaam jana mbele ya kikao cha watendaji wa Halmashauri za Manispaa ya Dar es Salaam na Wakili Mkuu wa Serikali, Anjella Kileo.Akisoma kanuni hizo, Anjella alisema kwa watengenezaji wa mifuko hiyo faini yake inaanzia Sh milioni 20 hadi Sh bilioni moja ama kifungo cha miaka miwili jela na kwa mtumiaji wa kawaida akikabiliwa na faini ya Sh 30,000 hadi Sh 200,000 ama kifungo cha siku saba.Kuhusu kanuni hizo, Anjella alisema Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Wakaguzi wa Mazingira anaweza kufifisha kosa lakini pia iwapo mkosaji atashindwa kuridhika na maamuzi ana uwezo wa kukata rufaa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) ndani ya siku 30.“Kwa mujibu wa kanuni ya nane, mwenye makosa atapelekwa mahakamani iwapo atakataa kosa na iwapo atakubali atapewa karatasi ya kulipa na kusaini lakini pia asiyeridhika na maamuzi ya Mahakama anaweza kukata rufaa kwa Mahakama za juu zaidi,” alisema.Alisema kwa yule ambaye hataridhika na ukaguzi wa Mkaguzi atakata rufaa kwa Waziri mwenye dhamana hiyo ndani ya kipindi hicho cha siku 30.“Kanuni hizi si sehemu ya kukusanya mapato, lengo ni mtu kuchagua kilicho bora na kizuri kwa ajili ya kulinda mazingira na afya kwa ujumla,” alisema Anjella.Alisema kanuni hizo zimebainisha baadhi ya bidhaa zilizosamehewa na kuendelea kutumika ikiwa ni pamoja na vifungashio vya dawa, vifungashio vya mabati, vifungashio vya bidhaa za kilimo, mifuko migumu ya taka na hata mifuko migumu ya kusindika vyakula.
3
HOMA ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga ambalo litapigwa kesho Jumamosi, imezidi kupanda, ambapo timu zote mbili zimejinasibu kwamba maandalizi kuelekea mchezo huo yamekamilika.Simba ambao ndiyo vinara wa ligi ni wenyeji wa mchezo huo, huku Yanga wakiwa wageni na mchezo huo umepangwa kupigwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuanzia saa 11:00 jioni.Uongozi wa klabu ya Yanga kupitia kwa Mhamasishaji wake, Antonio Nugaz, amezungumza na vyombo vya habari jana Makao Makuu ya klabu hiyo na kuwataka mashabiki wao kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kushuhudia kichapo ambacho wamekiandaa kwa ajili ya kuwapa watani zao Simba.“Mashabiki wa Yanga waondoe baridi waje uwanjani wakiwa wamevimba na kushuhudia tukichukua pointi tatu mbele ya Simba, kwasababu suala la kufungwa kwetu halipo, tumesajili vizuri, tumefanya maandalizi mazuri na nina hakika baada ya dakika 90 tutatoka kifua mbele,” alisema Nugaz.Mhamasishaji huyo alisema Yanga inayokwenda kukutana na Simba kesho ni nyingine siyo ya misimu miwili iliyopita na tayari wameziba mianya yote ya ujanjajanja waliokuwa wanafanyiwa na wapinzani wao Simba na kujikuta wakipoteza baadhi ya michezo, hivyo wao wamejiandaa kucheza mpira uwanjani na siyo nje ya uwanja.Alisema wameiandaa vizuri timu yao na watatoa pongezi kwa Simba endapo watacheza na kuzidiwa na Simba lakini siyo kuonewa kwa mambo mengine, ingawa pia wanawaheshimu waamuzi waliopangwa kuchezesha mchezo huo wa kesho wakiongozwa na Jonisia Rukyaa.“Simba wajue hii ni Yanga mpya ya Dk David Ruhago na Mshindo Msolla, tunataka kufungwa kimpira na siyo kimipango kama ilivyokuwa huko nyuma, tuna imani na kikosi chetu na leo (jana) kiungo Haruna Niyonzima amewasili tayari yupo kambini tutarajie kumuona uwanjani Jumamosi,” alisema Nugaz.Kiongozi huyo alisema Yanga kwa sasa haina njaa na tatizo la mishahara kama ilivyokuwa huko nyuma, hivyo hawana tena shida ya kuchangiwa fedha kwasababu wanazo za kutosha kutoka kwa wadhamini wao GSM pamoja na SportPesa.Aidha, Nugaz alisema kwa sasa wanafuatilia suala la beki wao, Lamine Moro, kama anaweza kucheza au kutocheza kwenye mchezo wa kesho kutokana na kuwa na kudaiwa kuwa na kadi tatu za njano, lakini alisema hata kama ikitokea beki huyo atakosekana wapo fiti kwasababu wamesajili wachezaji 30 kila nafasi ikiwa na wachezaji wawili hadi watatu.“Tuna mabeki wengi kwa nafasi anayocheza Moro, yupo Andrew Vicent Dante, yupo Ally Ally na Ally Sonso ni maamuzi ya kocha kuchagua amtumie yupi, lakini kwa jumla tupo vizuri kuhakikisha tunachukua pointi zote tatu kutoka kwa Simba,” alisema Nugaz.Yanga kwa sasa ina kamata nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 24, wakati Simba wakiwa ndio vinara kwa kujikusanyia pointi 34, wakifuatiwa na Azam FC iliyopo nafasi ya pili na pointi zao 26, lakini Yanga inafaida ya kuwa nyuma kwa mechi mbili dhidi ya timu hizo mbili za juu.
4
ERICK MUGISHA-DAR ES SALAAM HATIMAYE mfanyakazi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Tito Magoti (26) pamoja na mwenzake  ambaye ni mtaalamu wa Tehama, Theodory Giyani (36), wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu likiwamo la uhujumu uchumi. Magoti na mwenzake walifikishwa mahakamani jana na kusomewa mashtaka matatu likiwamo la utakatishaji fedha cha Sh milioni 17.3 kitendo ambacho ni kinyume cha sheria. Wakisomewa mashtaka hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Janeth Mtega pamoja na jopo la mawakili wanne wa Serikali. Hata hivyo Hakimu Mtega, alisema kuwa washtakiwa hao  hawatakiwi kujibu chochote kutokana na Mahakama ya Kisutu kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi za uhujumu uchumi isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka  nchini (DPP). Akisoma mashataka hayo mahakamano hapo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai kuwa Magoti na Giyani, wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 137/2019, huku akidai kuwa katika shtaka la kwanza, Magoti na Giyani wanadaiwa kushiriki genge la uhalifu. Kosa hilo wote wawili wanadaiwa kutenda, katika tarehe tofauti kati ya Februari Mosi na Desemba 17, 2019 jijini Dar es Salaam katika maeneo mbalimbali ya ndani ya nchi, ambapo Magoti, Giyani na wenzao ambao hawajafikishwa mahakamani, kwa makusudi wanadaiwa walishiriki makosa ya uhalifu ikiwa ni kumiliki programu za kompyuta iliyotengenezwa mahususi kwa ajili ya kufanya uhalifu. Hata hivyo Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi alidai katika shtaka la pili, washtakiwa hao na wenzao ambao bado hawajafikishwa mahakamani, wanadaiwa siku na eneo hilo, wanadaiwa kumiliki  programu za kompyuta kwa lengo la kutenda kosa la uhalifu. Na katika shtaka la tatu, ambalo ni kutakatisha fedha, Wakili wa Serikali Mkuu, Renatus Mkude, alidai Magoti na Giyani, wanadaiwa kutenda kosa hilo kati ya Februari Mosi na Desemba 17, 2019 katika Jiji la Dar es Salaam na maeneo mengine ndani ya nchi. Wanashtakiwa hao wanadaiwa katika tarehe hizo, wanadaiwa walijipatia Sh milioni 17.35 wakati wakijua fedha hizo ni zao tangulizi la kushiriki genge la uhalifu. Hata hivyo upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika  ambapo Hakimu Mtega aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 7, 2020 itakapokuja kwa ajili ya kutajwa. Washtakiwa wamerudishwa rumande kutokana na shtaka la kutakatisha fedha linalowakabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria. KUKAMATWA KWAKE Magoti alikamatwa Ijumaa Desemba 20, mwaka huu eneo la Mwenge  huku Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kilazimika kutaka kujua alilipo mtumishi wao hasa baada ya kumkosa kwenye vituo vya polisi jijini Dar es Salaam. Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alikiri kushikiliwa kwa Magoti na wenzake watatu ambapo hakueleza yupo kituo gani. Pamoja na jitihada mbalimbali za watendaji wa LHRC wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wao, Anna Henga kuzunguka katika vituo mbalimbali ikiwamo na kituo kikuu walijikuta wakigonga mwamba. Kutokana na hali hiyo juzi Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadami (THDRC) na Mtandao wa Wanawake Watetezi wa Haki za Binadamu (WHRDs) walifungua kesi Mahakama Kuu kumshtaki Mambosasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutaka walazimishwe kumpa dhamana.
3
NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM SIKU chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kutembelea Gereza la Butimba, Mwanza, Mahakama Kuu ya Tanzania imetoa waraka kwa majaji na mahakimu, ikiwataka kuhakikisha kesi zinazofikishwa mahakamani zinakidhi matakwa ya kisheria kuepuka msongamano wa mahabusi. Hivi karibuni, Rais Magufuli alitembelea gereza hilo na kuzungumza na wafungwa na mahabusi ambako alibaini changamoto lukuki huku suala la kubambikiwa kesi likiongoza kulalamikiwa na wengi. Waraka huo namba nne wa 2019, umetolewa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu, Dk. Eliezer Feleshi, kuhusu matakwa ya kuzingatia sheria katika ufunguaji na usikilizaji wa mashauri ya jinai mahakama kuu, mahakama za mahakimu wakazi na mahakama za mwanzo ili kuepukana na msongamano wa mahabusi usio wa lazima. Dk. Feleshi, alisema waraka huo umelenga kuwakumbusha majaji na mahakimu wajibu unaoendana na viapo vyao na kwamba watafuatilia utekelezaji wake. “Hakikisheni kesi zinazofikishwa mahakamani zinakidhi matakwa ya kusajiliwa kisheria na zinaposajiliwa hakikisheni mienendo hiyo inaendeshwa kwa kuzingatia matakwa ya sheria ambayo baadhi yametajwa hapo juu. “Hakikisheni kesi zinasikilizwa na kutolewa hukumu/uamuzi katika muda uliowekwa na sheria na kwa kuzingatia malengo ya mahakama,” alisema Dk. Feleshi. Kulingana na waraka huo, maelekezo mengine ni kutoa hukumu ndani ya siku 90 kuanzia siku jaji/hakimu alipokamilisha usikilizaji wa kesi husika na kupewa kipaumbele kwa adhabu mbadala ya kifungo cha jela kwa kufuata sheria. Pia majaji na mahakimu wameelekezwa kuhakikisha vikao vya kusukuma kesi vinafanyika kadiri ya waraka wa Jaji Mkuu Namba 2/1987 kama ulivyorekebishwa mwaka 2003 na 2011 na wachukue hatua zinazostahili kutekeleza maazimio yake. “Hakikisheni mahakama inashiriki kikamilifu kwenye vikao vya Jukwaa la Haki – Jinai ngazi zote na hakikisheni mwongozo wa ukaguzi unafuatwa kama ulivyo ikiwa ni pamoja na kuwafichua watumishi wa mahakama watakaotuhumiwa kwa vitendo vya rushwa. “Sambamba na hatua hiyo, vipo vikao vya Jukwaa la Haki – Jinai na vile vya kusukuma kesi ngazi za wilaya, mkoa na taifa ambavyo ni nyenzo za kuziwezesha mamlaka zinazohusika na utoaji wa haki – jinai kutatua changamoto zinazojitokeza katika ngazi mbalimbali katika nchi yetu,” alisema. Dk. Feleshi alisema pia endapo jaji au hakimu atajiridhisha kuwepo kwa vitendo vya hila vinavyohujumu mwenendo wa kesi iliyo mbele yake, mamlaka – asili ya kuondosha mashtaka na kumwachia huru mshtakiwa itabidi yachukue mkondo wake. Kwa upande wa wapelelezi na waendesha mashtaka, wamekumbushwa kutenda haki kwa kuzingatia Tangazo la Serikali namba 296 la 2012 linalotoa mwongozo kwa kesi nyingi isipokuwa zile zinazohusisha makosa makubwa ya kukamilisha upelelezi kabla ya kufunguliwa kwa kesi mahakamani. “Yapo maelekezo ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Novemba 3, 2008 ambayo kupitia kipengele cha nne yanaitaka mamlaka husika kumwajibisha mwendesha mashtaka au mpelelezi ambaye kwa hila atasababisha haki kutotendeka,” alisema Dk. Feleshi. UZINGATIAJI VIFUNGU VYA SHERIA Dk. Feleshi alisema Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai na sheria nyingine zinavyo vifungu vya sheria ambavyo kama vitazingatiwa magereza hayatalemewa na mahabusi. Alisema sheria hizo zina vifungu vinavyohusika na wajibu wa kutoa taarifa ya kutendeka kwa jinai au taarifa ya mpango wa kutendeka jinai. Hivyo waraka huo unasisitiza uzingatiaji wa vifungu vya sheria katika uandikishaji wa maelezo ya mlalamikaji na haki ya mtuhumiwa/mshtakiwa kupata maelezo ya mlalamikaji pamoja na hati ya mashtaka pale kesi inapofunguliwa mahakamani. Uandikishaji wa maelezo ya mashahidi mbalimbali wa mashtaka na yale ya washtakiwa, utaratibu wa kutolewa dhamana polisi kwa makosa yanayodhaminika pale ambapo polisi hawajakamilisha upelelezi. Utaratibu wa kutolewa kwa dhamana mahakamani kwa makosa yanayodhaminika kwa kufuata vigezo vya kisheria baada ya mtuhumiwa kufikishwa mahakamani. Utaratibu wa kuiomba mahakama isitoe dhamana kwa masilahi ya umma kwa kufuata misingi ya sheria na utaratibu wa kuwaweka wahalifu chini ya uangalizi wa polisi au mahakama bila kuwafungulia mashtaka na kuwafanya wakae mahabusu.
0
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso ameagiza Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Slyvester Mpemba kukamatwa na kuwekwa ndani baada ya kubaini fununu za ubadhirifu wa fedha katika mradi wa maji uliopo kata ya Mwakitolyo.Aidha amemtaka kaimu Mhandisi wa maji mkoa wa Shinyanga, Julieth Payovelo kujieleza ni kwa nini asifukuzwe kazi, huku akieleza kushangazwa na kitendo cha mkandarasi kupewa Sh bilioni 1.462 na mradi huo kutokamilika kwa wakati.Aweso ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Mwakitolyo.Aliwaeleza wananchi kuwa serikali imekwishatoa fedha zote Sh bilioni 1.482 ambazo waliziomba na kudai mradi huo utakamilika."Niliwauliza wananchi mradi huu utaweza kugharimu kiasi gani hadi kukamilika lakini majibu yao yalikuwa ni zaidi ya Sh bilioni 1.4, fedha hizo zote wamekwisha mlipa mkandarasi na mradi kutokamilika kwa kipindi cha miaka minne sasa," alisema na kuongeza:"Waliomba tena kwa andiko Sh milioni 180 ili wakamilishe mradi huo ambazo fedha hizo zitoke kwenye mabaki ya miradi mingine, lakini kama nasema uongo mhandisi akiri kuomba Sh milioni 120 tena ambayo imenipa mashaka kama hazikutosha zile nyingi hizi chache zitaweza kutosheleza?".Aweso baada ya kumuita mbele ya wananchi mhandisi wa maji, Mpemba alikiri kupewa fedha hizo na kwamba mradi hautoi maji.Aliwaita askari wamkamate na kumuweka ndani huku akimuagiza mhandisi wa maji mkoa, Payovelo kujieleza zaidi.Mbunge wa Solwa, Ahmed Salum alishukuru hatua aliyochukua naibu waziri huku akieleza kuwa mradi huo umekuwa ukimtesa.Alisema alikuwa anakosa majibu mbele ya wananchi waliokuwa wakimuuliza kuhusu kuondoa changamaoto ya upatikanaji wa maji safi. Mwenyekiti wa kijiji cha Mwakitolyo, Nuru Shoni alisema kuna wakazi zaidi ya 22,000.Alisema kuwa naibu waziri alikuja Januari mwaka jana akaahidi kutekeleza mradi baada ya kuwakuta akina mama wamepanga ndoo zao barabarani na kuahidi kero hiyo ataiondoa.Mkazi wa kijiji cha Mwakitolyo, Saada Hamis alisema kero ya maji inawalazimu kununua dumu la maji Sh 1,000.Mradi huo unatekelezwa na kampuni ya Helam Construction ambayo iliingia mkataba mwaka 2014, lakini kilichobainika maji hayatoki na wananchi wanashindwa kupata huduma.
3
WINFRIDA MTOI Na ASHA KIGUNDULA – DAR ES SALAAM TIMU ya Yanga imeondoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Mara, ambako itakabili Biashara United, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Uwanja wa Karume mjini Musoma. Kwa upande mwingine, wapinzani wa Yanga, timu ya Simba nayo iliondoka jana hiyo hiyo jijini humo kwenda mkoani Mtwara, kwa ajili ya mchezo waje na Ndanda utakaochezwa Uwanja wa Nangwanda, Sijaona. Timu hizo kila moja itacheza michezo miwili zikiwa huko kwa maana ya Yanga Kanda ya Ziwa na Simba Kanda ya Kusini. Yanga baada ya kuivaa Biashara United, Wanajangwani hao wataelekeaBukoba, kuikabili Kagera Sugar dimba la Kaitaba. Simba ikimalizana na Ndanda itasafiri hadi Lindi ambako itapepetana na Namungo Uwanja wa Majaliwa. Baada ya mchezo na Namungo, Wekundu hao litafuatia tukio la Wekundu hao kukabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu. Simba imefanikiwa kutwaa ubingwa huo, baada ya kufikisha pointi 79 katika michezo 32, licha ya kusaliwa na michezo sita kabla ya msimu kufikia tamati. Kigezo kilichoipa ubingwa ni washindani wengine 19 wanaoshiriki ligi hiyo kutokuwa na uwezo wa kufikisha pointi hizo, hata kama watashinda michezo yao yote waliyobakiwa nayo. Baada ya ziara zao Kanda ya Ziwa na Kusini, Simba na Yanga zitarejea Dar es Dalaam kabla ya kuumana Julai 12 katika pambano la nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Tanzania maarufu Kombe la Azam(ASFC). Meneja wa timu ya Yanga, Abed Mziba, alisema wameondoka na wachezaji 24, akiwemo Bernard Morrison huku walibaki Dar es Salaa ni wale majeruhi kama Papy Tshishimbi. Alisema Morrison ameambatana na wenzake baada ya kumaliza tofauti kati yake na klabu hiyo ikiwemo kuwaomba msamaha wachezaji wenzake. “Timu imeondoka na wachezaji 24, mechi tulizonazo ni ngumu tunahitaji kuwa na kikosi kipana, waliobaki Dar es Salaam ni wa majeruhi pekee,”alisema Mziba. Naye Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu, alisema wamesafiri na kikosi chao chote kwakua wakiwa Ruangwa mkoani Lindi watakuwa na hafla ya makabidhiano ya kombe. Alisema wameelekea Kusini wakiwa na vitu viwili vya kufanya, kuhakikisha wanachukua pointi zote sita na kusherehekea ubingwa wao. “Tumeondoka Dar es Salam alifajiri, wachezaji wote wapo katika hali nzuri, tuko tayari kwa mapambanpoi pamoja na sherehe zetu za kukabidhiwa kombe,” alisema Rweyemamu.
4
ACCRA, GHANA MFANYAKAZI mmoja wa kiwanda cha samaki nchini Ghana, amewaambukiza kirusi cha corona kinashosababisha maradhi ya Covid-19 wafanyakazi wenzake 533 wa kiwanda hicho. Hayo yameelezwa na Rais Nana Akufo-Addo katika hotuba kwa taifa jana na kusisitiza kuwa, watu wote hao 533 waliambukizwa virusi vya corona na mtu mmoja.  Hata hivyo hakutoa ufafanuzi ni vipi  ugonjwa huo wa Covid-19 ulienea kiwandani humo na kama hatua za tahadhari za kiafya zimechukuliwa kufuatia maambukizi hayo. Kwa mujibu wa Rais Akufo-Addo, maambukizi hayo ya watu 533 waliothibitika kuwa na virusi vya corona, ikiwa ni takribani asilimia 11.3 ya maambukizo yote ya nchi nzima ni sehemu ya kesi mpya 921 za watu waliobainika kuambukizwa ugonjwa wa Covid-19 katika kipindi cha karibu wiki mbili zilizopita ambazo takwimu zake zimetolewa hivi karibuni. Katika hotuba yake hiyo ya jana, Rais wa Ghana alirefusha tena marufuku ya mikusanyiko ya umma hadi mwishoni mwa mwezi huu wa Mei huku shule na vyuo vikuu nchini humo vikiendelea kufungwa. Mamlaka za Afya za Ghana ziliripoti siku ya Ijumaa kuhusu mripuko huo wa maambukizo ya corona katika kiwanda hicho cha samaki kilichoko kwenye mji wa kando ya bahari wa Tema lakini hazikutoa maelezo zaidi. Maambukizo mapya ya corona yaliyotangazwa jana yameifanya Ghana kuwa na jumla ya watu 4,700 wenye virusi vya corona tangu mripuko wa janga hilo lililoikumba dunia nzima ulipotangazwa nchini humo kwa mara ya kwanza katikati ya mwezi Machi. Takwimu za jana zimeifanya Ghana kuwa nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu walioambukizwa virusi vya corona katika eneo la Afrika Magharibi. Hadi sasa watu 22 wamefariki dunia kwa maradhi ya Covid-19 nchini humo na wengine 494 wamepata afueni.
2
NA SHOMARI BINDA-RORYA WAZEE wa Wilaya ya Rorya mkoani Tarime, wamelalamikia vitendo vinavyofanywa na vijana kwa kuchukua hatua ya kuwachapa viboko kwa kile kinachodaiwa kuendeleza mila potofu ambazo pia zimekuwa zikiwadhalilisha na kuendeleza ukatili. Wakizungumza kwenye semina iliyoandaliwa na shirika la Masister wa Moyo Safi wa Maria Afrika na kuwashirikisha wazee wa mila wa wilaya hiyo katika kampeni ya kupambana na ukatili wa kijinsia, walisema maadili kwenye jamii yamepungua na ndiyo kunapelekea kuendelea kwa vitendo vya ukatili. Walisema si wanawake pekee wanaofanyiwa ukatili bali hata wazee pia wamekuwa wakifanyiwa hivyo kwa kuendeleza mila za kuwachapa viboko pale wanapodaiwa kutenda kosa jambo ambalo wamedai linawadhalilisha na ni moja ya ukatili wanaofanyiwa. Mmoja wa wazee hao aliyejitamulisha kwa jina la Andrecus Nyazam wa Kijiji cha Kwibuse, alisema zipo taratibu za kufuata pale mtu anapokuwa amekosa kwenye jamii lakini si vijana kuchukua hatua ya kuwachapa wazee viboko. Alisema mila hiyo ni ya ukatili sawa na ule ambao wamekuwa wakifanyiwa wanawake kwenye jamii na kudai elimu bado inapaswa kuendelea kutolewa zaidi ili kuachana na mila ambazo zimekuwa kikwazo. “Tunashukuru kwa semina hii ambayo tumeshirikishwa ili kwa pamoja tuweze kuimarisha haki za wanawake walioathiriwa na ukatili wa kijinsia kwenye maeneo yetu lakini na sisi wazee tumekuwa na kilio chetu cha kudhalilishwa na kufanyiwa ukatili na vijana kwa kuchapwa viboko. “Tunakwenda kutoa elimu kwa jamii juu ya kuachana na vitendo vya ukatili kwenye jamii zetu tunaomba pia sauti zisikike za kukemea mila zisizofaa ambazo kwa kiasi kikubwa ndio chanzo cha ukatili unaokuwa unatendeka,”alisema. Mratibu wa mradi wa kuimarisha haki za wanawake walioathiriwa na ukatili wa kijinsia unaotekelezwa kwenye Kata 13 za Wilaya ya Rorya, Nollasko Mgimba, alisema jamii inapaswa kuweka mpango wa kutokomeza mila ambazo hazifai kwenye jamii. “Pamoja na ukweli kwamba mila zina umuhimu wake mkubwa katika jamii, lakini tunapaswa kubadilika na kuachana na mila zisizofaa kulingana na maendeleo ya kijamii hasa katika nyanja za kiuchumi na kijamii,” alisema. Mwisho
3
Mapenzi ni sawa na gurudumu, ni lazima kutiwa nishati ili kubingiria Mapenzi ni gari, huelekea anakotaka dereva, mapenzi mto hufuata mkondo Katika kila uhusiano, upo wakati ule wa kwanza mpokutana na kuamua kuwa meli hii tunakubali kuipeleka ndumakuwili, basi yapo baadhi ya mambo ambayo kila anayetosa katika bahari la penzi hupaswa kujihadhari nayo. Haya ni baadhi ya makosoa ambayo hupaswi kufanya unapokutana na demu kwa mara yakwanza: 1. Kuchelewa. Unapokutana na mume au mke kwa mara ya kwanza usidhubutu kuchelewa. Ikiwa kuna jambo la dharura ambalo lazima linakuchelewesha basi jambo la heri ni kutuma arafa na kujieleza kwa mepema. 2.Kuuliza maswali. Unapomuuliza mtu maswali, anakuwa na Imani nawe. Katika kuuliza maswali, unapaswa kuwa makini ili kutouliza ama kuyajibu maswali ambayo hayafai maana maswali mengine huweza kuwa mtego. 3.Kuzungumza kuhusu mpenzi wa zamani. Usingumze lolote kumhusu mpenzi wa zamani ila unapoulizwa. Unapoongea kumhusi, inaonyesha wazi kuwa ungali na hisia zake na kuwa hupo tayari kusonga mbele. 4.Kuangalia simu. Unapoangalia simu yako kila wakati, unaweza kutatizwa ama kujihusisha kwa mambo mengine yasiyohusu mkutano wenu na hata kugeuza nia zima. 5.Kuzungumza kupita kiasi. Hakikisha kuwa mazungumzo yako yanatiririka na wala huibua masuala yasiyohusu mkutano wenu. Iwapo mlo naye hazungumzi, jaribu kumuuliza maswali mengine ya balagha. 6.Kujishaua kuhusu mapato yako, kazi na kisomo. Kwa jumla si vizuri kujishaua unapokutana na mtu kwa mara ya kwanza, ijapokuwa una kisomo ama utajiri mkubwa, inakuwa vyema hayo yanapotambulika baada ya muda. Kunao wale ambao wataanza kukuambia eti wajua nimetoka ng’ambo jana na mambo kama hayo, hayafa kamwe.
1
TAASISI ya kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Geita katika kipindi Oktoba hadi Desemba, mwaka jana, imeokoa zaidi ya Sh milioni 16 za taasisi mbalimbali ikiwamo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)ambazo zingehujumiwa.Taasisi hiyo imepokea malalamiko ya rushwa 48 kutoka kwa wananchi ambapo malalamiko 10 kati yake yamefunguliwa majalada ya uchunguzi na mengine uchunguzi umekamilika na nane yamepelekwa makao makuu kwa ajili ya hatua zingine.Aidha, Takukuru Mkoa wa Geita imeanza uchunguzi kwa kasi kupitia timu maalumu iliyoundwa inawaoshirikisha watalaamu kutoka sekta tofauti wakiwemo maafisa wa Takukuru kuhusu matumizi ya fedha za miradi ya maendeleo zilizotokana na fedha za huduma za kijamii CSR kutoa mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) ambapo baadhi ya watumishi wa mgodi wameanza kuhojiwa.Mkuu waTakukuru Mkoa wa Geita Thobias Ndaro alisema hayo juzi wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi wa taasisi hiyo katika kipindi cha miezi mitatu kutoka Oktoba hadi Desemba, mwaka jana, ofisini kwake alipokuwa akizungumza na wanahabari.Ndaro amesema, Sh milioni15 kati ya Sh milioni 16. 6 zilizookolewa zilitokana na kukamatwa kwa mfanyabiashara wa kuuza simu na vifaa vya simu katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro aliyekamatwa kwa kukwepa kulipa kodi wakidaiwa kushirikiana na baadhi ya watumishi wa TRA.Mfanyabiashara huyo alikamatwa wakati wa ujio wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na baada ya uchuguzi wa kina ilibainika kuwa kweli na kutozwa kodi ya Sh milioni 15 na uchunguzi dhidi yake ulikuwa bado unaendelea kwa kuangalia rekodi zake za nyuma.Kiasi kingine cha fedha kilichookolewa kilitoka Idara ya Elimu Sh 200,000 na Idara ya polisi kutoka wilaya ya Bukombe Sh milioni 1.1 na Sh 313,000 ziliokolewa kutoka wilayani Chato katika Idara za Elimu, Madini na Ardhi.Mbali na kuokoa fedha hizo Takukuru mkoa wa Geita imeanza kutekeleza kwa kasi uchunguzi wa matumizi ya fedha za miradi ya maendeleo ya kijamii kutoka mgodi wa Geita kupitia CSR ambapo tayari watu kadhaa wakiwemo watumishi wa GGM wamehojiwa.
3
Pia amewataka wachezaji wa timu hiyo kuheshimu maadili ya michezo kwa kutojihusisha na matendo ya utovu wa nidhamu badala yake kuwa na dira ya mafanikio.Kikwete alitoa wito huo jana alipozungumza na wachezaji na viongozi wa timu hiyo walioenda kumtembelea Ikulu na kumkabidhi Kombe la Kagame walilolitwaa mwishoni mwa wiki iliyopita kwa kuifunga Gor Mahia ya Kenya mabao 2-0.Kikwete alisema kuwa Azam imekata kiu ya Watanzania kwa kuwaletea kombe kubwa kama hilo na kuwataka kutobweteka.Alisema kuwa Azam Fc ni moja kati ya klabu ambazo zinaonekana kujipanga na kupambana na klabu kubwa hasa katika medani ya soka kwa kuwa imejipatia umaarufu na mafanikio makubwa katika soka kwa muda mfupi. Alisema kuwa Watanzania wanapenda soka ingawaje wanakwazwa na mambo mbalimbali ambayo yanarejesha nyuma tasnia hiyo.“Azam ni klabu ambayo binafsi naona kuwa inaweza kufika mbali zaidi katika soka hasa kutokana na kuwa na umakini wakati imeanzishwa na hadi leo hii inachukua kombe kubwa kama hili la CECAFA, hii ni ishara ya kuwa kama Tanzania ikiwekeza zaidi basi siku moja tutakuwa mbali katika soka,” alisema Kikwete.Aliwataka kuhakikisha kuwa wanashinda Kombe la Shirikisho Afrika michuano ambayo timu hiyo itashiriki mwakani na kuendelea kuwapatia furaha Watanzania na kusema kuwa klabu hiyo inaweza kufanikisha hilo. Pia alipata wasaa wa kubadilishana mawazo na wachezaji hao akiwa eneo la nje ambapo alisikika akiwataka kuzingatia zaidi mazoezi na kuepuka vishawishi.“Mimi nawaambieni nyie vijana kuna mengi huko mtaani utakuta unapitapita mitaani na kisha unaitwa na watu wanakukaribisha kinywaji, sasa ukijisahau unaweza kujikuta unaanza kupotea njia na kuwa mlevi na kushindwa kuendelea na soka,” alisema Kikwete.Aliongeza kuwa: “Kamwe msikwepe kufanya mazoezi bila ya sababu za msingi manake sio wakati wa mazoezi wewe unaitiwa mambo binafsi yasiyokuwa na faida kwa soka na unapotelea huko hiyo sio nzuri”.Aliwata wachezaji hao kutumia muda wao mwingi kusoma vitabu kutoka kwa wachezaji wengine waliofanikiwa na kuiga mazuri kutoka kwao.Rais Kikwete pia alikabidhiwa jezi namba tisa kutoka kwa Mwenyekiti wa timu ya Azam, Said Mohamed ambapo alisema kuwa klabu hiyo imeamua kumkabidhi jezi yenye namba hiyo kwa kuwa ni namba ya mashambulizi.Awali akimwelezea madhumuni ya ujio wao Ikulu, Mohamed alisema kuwa timu hiyo imeamua kwenda Ikulu kumuonesha kombe hilo Rais kutokana na hamasa ambayo Kikwete aliwapa wakati akifungua Uwanja wao wa Azam Complex uliopo Chamanzi, Dar es Salaam.Alisema kuwa katika kuhakikisha timu hiyo inafika mbali ilijipanga na kuchukua taji la Ligi Kuu msimu wa 2013/ 2014 na msimu wa mwaka 2014/20 15 ikawa ya pili. Aliongeza kuwa baada ya hapo ikahakikisha kuwa inachukua kombe jingine kubwa zaidi ambalo ni CECAFA na ndio imelipeleka kwa Rais kama zawadi yao kwake.“Mheshimiwa leo tumeleta zawadi hii kwako na ni matunda ya hamasa yako haya, sasa basi tunakuhakikishia kuwa kazi ndio inaanza kwa kuwa tunataka kuleta kombe kubwa la Shirikisho Afrika, CAF,” alisema Mohamed.
4