text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
Mei 5, mwaka huu Tanzania iliungana na mataifa mengine duniani kusherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wakunga Duniani ambayo kwa mwaka huu yalipewa Kauli mbiu isemayo ‘Wakunga ni Chachu katika Utoaji Huduma bora kwa mama na mtoto’. Tanzania iliadhimisha siku hii ya pekee, maadhimisho hayo yalifanyika huko mkoani Morogoro katika viwanja vya sabasaba. Upo msemo wa wahenga usemao, usitukane wakunga na uzazi ungalipo, msemo huu unalenga kuhamasisha jamii kumthamini mkunga kulingana na nafasi yake nyeti aliyonayo. Mkunga ni mtu muhimu mno katika kusaidia kufanikisha kuanza kwa safari ya mwanadamu duniani, huhitajika katika kusaidia na kufuatilia hali ya mama tangu anapogundulika kuwa mjamzito, kipindi cha ujauzito na hadi kujifungua. Hata baada ya mama kujifungua, mkunga huendelea kufuatilia hali yake na mtoto au watoto waliozaliwa hadi wanapofikisha kipindi cha umri wa miaka mitano. Zamani mabibi zetu walilazimika kujifungua kwa msaada wa wakunga wa jadi ingawa hadi sasa bado zipo jamii ambazo hujifungua kwa wakunga hao. Hata hivyo, kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia wengi leo hii wanajifungua kwa msaada wa wakunga wataalamu. Pamoja na umuhimu wao, baadhi ya wakunga kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakilalamikiwa na wananchi wakiwamo wajawazito, kwamba wanatenda kazi bila kuzingatia misingi ya taaluma yao. Wapo ambao wanatuhumiwa kuwatolea lugha zisizofaa wajawazito wakati wanapokuwa wakiwahudumia huko kliniki au katika vyumba vya kujifungua (labour). Simulizi ya Frida Frida Eliud Mkazi wa Morogoro ni mama wa watoto wawili, anasema mtoto wake wa kwanza alijifungulia katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro mwaka 1998. Anasema wakati wa ujauzito wake huo wa kwanza alipatwa wasiwasi mwingi wa kuanza kuhudhuria kliniki hasa alipokuwa akikumbuka simulizi alizosimuliwa na wanawake wenzake kuhusu lugha zinazotolewa huko kliniki. “Walikuwa wakinisimulia jinsi walivyopokelewa katika hospitali walizokwenda, kwamba baadhi ya wakunga na wauguzi wanatoa lugha za kuudhi. Lakini ilifika mahali nikasema wacha niende tu kwa sababu sina jinsi na lazima nifuatilie maendeleo ya hali yangu na mtoto wangu aliye tumboni. “Nilianza kuhudhuria kliniki, sitasahau siku ile ya kwanza, muuguzi aliyenipokea hakuwa na lugha nzuri, hata siku nilipokwenda kujifungua mkunga aliyenisaidia naye hakuwa na lugha nzuri, kusema ukweli wapo wanaofanya vema lakini kuna wengine wanawaangusha kwa kufanya yasiyofaa. “Kila nilipomuita aje anisaidie alikuwa akiniambia nisimsumbue, kwamba kuna wengine pia waliokuwa wakihitaji kusaidiwa na yeye hakuwa na uwezo wa kujigawa atusaidie wote. “Nilihangaika usiku kucha sikufanikiwa kujifungua hadi ilipofika asubuhi, mume wangu alikuja nikamsimulia kilichokuwa kikiendelea. “Alisikitika mno lakini hakuwa na jinsi, ilibidi wasubiri hadi nilipojifungua majira ya saa nne hivi, tukarudi nyumban,” anasema. Anasema kuwa ujauzito wake wa pili akaamua kwenda tena hospitali nyingine ya serikali, akapokelewa na mkunga wa kiume, nilichelewa kujifungua lakini aliendelea kunihudumia kwa upendo na kwa kunithamini mno. Anasema alikuwa akimtia moyo na kumtaka asiogope, kwamba nitajifungua salama. Mama mwingine Mariam James (50) Mkazi wa Morogoro Mjini ni mama wa watoto watatu, anasema awali alikuwa akiishi jijini Dar es Salaam eneo la Sinza kwa Remmy. Anasema alipojihisi kuwa ni mjamzito, mwaka 1990 aliamua kufanya uchunguzi hospitali ipi itamfaa kwa huduma ya kliniki. “Wanawake wenzangu walishanisimulia changamoto walizokumbana nazo katika hospitali mbalimbali, lakini nikasema kwa kuwa ninahisi ni mjamzito nifanye uchunguzi kwanza hospitali ipi itanifaa nianze kliniki. “Basi nilikwenda kwanza Hospitali ya Tandale, nikakaa kwenye benchi nikaangalia namna ambavyo wauguzi na wakunga walivyokuwa wakipokea wagonjwa na kuzungumza nao,” anasema. Anasema hakuridhishwa na watumishi wa hospitali hiyo, hivyo aliondoka tena hadi Hospitali ya Mwananyamala akakaa kwenye benchi na kufanya tena uchunguzi wake. “Hapo napo sikuridhika na huduma, nikaondoka hadi Hospitali ya Mnazi Mmoja nikafanya hivyo hivyo, kidogo hapo niliridhishwa na huduma, kulikuwa na wauguzi na wakunga wenye umri wa utu uzima tofauti na kule nilipokwenda awali, walikuwa wakipokea watu kwa kauli nzuri mno. “Lakini nikasema ngoja niende na Hospitali ya Taifa Muhimbili nikaangalie huduma zilivyo, huko sikuridhishwa, nikaamua kurudi Mnazi Mmoja wale watumishi wakaniambia muda ulikuwa umekwisha, ilikuwa siku ya Ijumaa basi wakanishauri niwahi mapema asubuhi nianze kliniki,” anasema. Mariam anasema aliondoka akiwa na furaha na kwamba aliwahi mapema Jumatatu hospitalini hapo na kuanza kliniki ya uzazi. “Wale watumishi walikuwa wakiongea nasi kwa lugha nzuri, walikuwa wanahudumia kwa upendo, wanafariji na wanabembelea mtu unajisikia amani muda wote tofauti na wale watumishi wa hospitali zingine ambazo nilikwenda walikuwa wakizungumza vibaya na wagonjwa. “Niliendelea kuhudhuria kliniki Mnazi Mmoja lakini nilipofikia kujifungua walinishauri nitafute hospitali nyingine kwa sababu wakati ule pale walikuwa hawana huduma ya kujifungua bali ya kliniki tu. “Ingawa nilitamani kujifungulia pale lakini sikuwa na jinsi ilibidi nirudi Mwananyamala nikajifungulia hapo, kusema ukweli jinsi wauguzi na wakunga wenye umri wa utu uzima walivyokuwa wanahudumia ilikuwa tofauti kabisa na wale wenye umri wa ujana wakati huo,” anabainisha. Anasema hadi sasa anaona kuna tofauti kubwa kati ya watumishi wenye umri mkubwa jinsi wanavyohudumia wagonjwa na wale wenye umri mdogo. “Wenye umri mkubwa wana hudumia kwa upendo zaidi kuliko hawa vijana, kwa msingi huo, ikiwa inawezekana basi naishauri serikali iangalie hii kazi ya uuguzi na ukunga ifanywe na watu wenye umri wa utu uzima kuliko vijana,” anashauri. Ukweli wa mambo Pamoja na umuhimu wa kada hii katika sekta ya afya, kwa muda mrefu sasa yamekuwapo malalamiko kutoka kwa jamii wakidai baadhi yao wamekuwa wakizungumza lugha zisizofaa (kejeli au matusi) kwa wajawazito hasa wanapokwenda kujifungua. Hivi karibuni, tulishuhudia jinsi ambavyo ‘sekeseke’ hilo lilipamba moto kiasi cha baadhi ya viongozi wa serikali kuonekana waziwazi wakiwachukulia hatua wauguzi na wakunga waliodaiwa kutoa lugha zisizofaa kwa wagonjwa kwa kuwaweka rumande. Hata hivyo, ililazimu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kutoa tamko la kuwataka viongozi wa serikali kuziachia mamlaka zinazosimamia maadili ya kitaaluma kuwachukulia hatua watumishi hao kwa kufuata misingi ya sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa. Pamoja na hayo, inadaiwa watumishi wengi wa kike wa kada hizo ndiyo ‘vinara’ wa kutoa lugha chafu kwa wajawazito tangu wanapohudhuria kliniki na hadi kipindi cha kujifungua kuliko watumishi wa jinsia ya kiume. Rais wa Chama cha Wakunga Tanzania (TAMA). Feddy Mwanga, anakiri kwamba wamekuwa wakipokea malalamiko kutoka kwa jamii dhidi ya baadhi ya wakunga. “Wapo wanaotuhumiwa kutoa lugha zisizofaa na tunapopokea malalamiko tunafuatilia kwa ukaribu na ambaye anakutwa na hatia tunamchukulia hatua kwa mujibu wa sheria,” anabainisha. Utafiti wafichua mambo Maurice Hiza ni Ofisa katika Idara ya Huduma na Ukunga wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, anasema waliamua kufanya uchunguzi wa kina juu ya malalamiko hayo. “Tulipokea malalamiko mengi mno na tukaamua kufanya uchunguzi wetu wa kina ili kujua je, ni kweli au watu walikuwa wakieneza tu uvumi, baada ya uchunguzi wetu tulibaini ni kweli wapo baadhi ya wakunga ambao hutamka lugha zisizofaa wanapokuwa wakihudumia wateja,” anasema. Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubsya anasema wizara ina utaratibu maalum wa kushughulikia kero zinazowapata wafanyakazi wake. Anasema taratibu hizo zinaendana na sheria za nchi na zimewekwa mahususi kuzishughulikia kero zozote ziwe zimesababishwa na mazingira ya kazi, wafanyakazi wenzao au watu wanaokuja kupata huduma. “Mara nyingi tunaweza kuwa tunashughulika na watu wanaotoa huduma baada ya wafanyakazi kuja kutoa taarifa kwamba wamefanyiwa jambo fulani au mtu ameona mfanyakazi amefanyiwa jambo akatupa taarifa na sisi tunafuata utaratibu. “Tunauliza mfanyakazi amefanyiwa jambo gani na lazima tumjue aliyefanya jambo husika, hatua hii imetusaidia mno kutatua kero mbalimbali za wafanyakazi, vile vile mahali pa kazi ni salama kwa sababu ya utaratibu tuliojiwekea wa ndugu, namna ya kuingia katika maeneo ya kazi hata wagonjwa wenyewe. “Kwa hiyo, hatutegemei wakunga wanaweza kudharauliwa, kutukanwa na ndugu kwa mazingira ya kawaida ya kazi kwa sababu anaposhughulika na wajawazito kuna utaratibu wao ambao wanausimamia,” anasema. Dk. Ulisubisya anasema hata hivyo, pamekuwa na malalamiko na mengi huyapokea kutoka kwa ndugu wa wagonjwa kulalamikia huduma zinazotolewa hasa kuhusu lugha. “Hilo tumekuwa tukilishughulikia kwa kuhakikisha tunakuwa na huduma rafiki katika maeneo yote,” anabainisha. Wakunga wafunguka Wakati jamii ikilalamika na kuwatuhumu baadhi ya wakunga kutotimiza wajibu wao kwa mujibu wa misingi ya taaluma yao. Wakunga nao wamefunguka na kutoa yale yaliyo moyoni mwao ambapo hapa wanaeleza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wakati wa kutekeleza majukumu yao ya kila siku. Akizungumza na MTANZANIA Mariam Japhet, Mkunga wa Hospitali ya Ulanga mkoani Morogoro, anasema amefanya kazi hiyo tangu mwaka 1990 na kwamba amekutana na mikasa mingi. “Nakumbuka kuna siku nilipokea mjamzito ambaye mapigo yake ya moyo na ya mtoto yalionekana kushuka mno, nilimjulisha daktari aliyekuwa akimfanyia vipimo zaidi, yule mama alibaini mtoto alikuwa tayari amefariki dunia. “Alipofanyiwa upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni, alikutwa na tatizo la kichwa kikubwa, basi ndugu aliyekuwa amekuja na mgonjwa alijulishwa lakini alipokuja mumewe hakuwasilisha vizuri maelezo yale aliyopatiwa,” anasema. Anasema hali hiyo ilisababisha baba wa mtoto husika na baadhi ya ndugu kuanza kulalamika kuwa mtoto wao alikuwa amefariki kutokana na uzembe. “Ikabidi tutumie ujasiri kumuita baba husika na kumuonesha ule mwili wa mtoto wake alipoangalia na kuona alikuwa na tatizo la kichwa kikubwa aliamini hakukuwa na uzembe uliokuwa umefanyika,” anasema. Muuguzi mkunga mwandamizi, Agnes Mtawa ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Msajili wa Baraza la Wakunga Tanzania anasema katika miaka zaidi ya 20 aliyohudumu katika fani hiyo amepitia mambo mengi. “Katika hospitali niliyokuwa nasimamia, kuna siku aliletwa mjamzito ambaye alifikishwa akiwa amechoka mno na bahati mbaya mtoto alifariki tukiwa zamu ya usiku tutachukua kitenge chake tukamstiri mtoto. “Ndugu walipokuja asubuhi wakabaini kitenge hakikuwepo wakadai kwamba kilikuwa kimeibiwa na wakunga tuliokuwa usiku ule, kwa haraka haraka tulikubaliana tulipe. “Lakini tulifanya jitihada kuangalia kilienda wapi, tukakagua na kubaini kwamba tulimfungia mtoto baada ya kufariki dunia, ndugu walikuwa tayari wamekasirika hawakuwa na uchungu tena na kifo cha mtoto wao walikuwa na uchungu na kile kitenge. “Kwa kawaida tulikubaliana kwamba mama akiletwa pale hospitalini (Muhimbili) kila kitu chake alichokuja nacho lazima kiandikwe anapoingia na anapotoka, na hatua hiyo ndiyo ilitusaidia kujua ukweli kwamba kitenge hakikupotea bali alifungiwa mtoto kumsitiri,” anasema. | 0 |
WAZALISHAJI na wasambazaji wa taulo za kike wametakiwa kuunga mkono juhudi za serikali na wadau wengine kuwamkomboa wasichana dhidi ya vikwazo mbalimbali vya kielimu kwa kutopandisha bei ya bidhaa hizo.Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Chama Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa), Joyce Shebe alieleza kusikitishwa na hatua ya wazalishaji kushindwa kupunguza bei licha ya serikali kuwafutia Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika mwaka wa fedha 2018/19.Kutokana na kitendo hicho, katika Bajeti Kuu ya mwaka 2019/20 iliyosomwa mwishoni mwa wiki, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amependekeza msamaha huo kufutwa.“Wafanyabiashara na wa- zalishaji wote ni wazawa na wadau wanaopaswa kuunga mkono juhudi za serikali kumkomboa mtoto wa kike. Sote tungeunganisha nguvu ili mtoto wa kike aweze kupata elimu,” alisema.Alisema lengo la serikali halikuwa kuwaneemesha wafanyabiashara pekee, hivyo walipaswa wazingatie kwamba wao pia wanapaswa kutoa mchango wa kumwendeleza mtoto wa kike kwa kupunguza gharama za taulo hizo. Kiongozi huyo wa Tamwa alishauri wafanyabi- ashara kutopandisha bidhaa hiyo katika mwaka ujao wa fedha kwa kigezo cha kufidia msamaha uliofutwa.Uamuzi wa serikali kuwafutia wazalishaji wa taulo za kike VAT katika mwaka wa fedha 2018/19, ulilenga kuitikia kilio cha makundi mbalimbali, ikiwamo Tamwa waliotaka bidhaa hiyo muhimu ipatikane kwa bei nafuu kwa ajili ya kulinda afya ya mama na mtoto wa kike hasa walio shuleni. Wabunge ni kundi lingine lililopaza sauti na kushauri serikali kupunguza kodi bidhaa hizo ziuzwe kwa bei ya kawaida.Hata alipokuwa akisoma bajeti, Waziri Mpan- go alisisitiza kwamba matarajio ya serikali ni kuona wazalishaji na wauzaji wa taulo za kike wanaziuza kwa bei nafuu baada ya kusamehewa kodi hiyo; jambo ambalo halikutekelezwa. | 3 |
Mwandishi wetu, Tanga MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema kampeni ya elimu kwa mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) itawasaidia wafanyabiashara wanaokwepa kodi kuacha vitendo hivyo vya kuikosesha Serikali mapato. Shigela ameyasema hayo ofisini kwake alipotembelewa na maafisa wa TRAwanaofanya kampeni hiyo mkoani humo ambayo imelenga kuwaelimishawafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati. Amesema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi pengine kwa kujua au kutokua, jambo ambalo linahitaji elimu ya uelewa ili kila mwananchi afahamu wajibu wake kwenye ulipaji wa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Akiizungumzia kampeni hiyo, Shigela ameipongeza TRA kwa kuendesha zoezi hilo katika mikoa mbalimbali na kusema litaongeza ukusanyaji wa mapato baada ya wafanyabiashara kuelimishwa na kufahamu kuwa maendeleo ya nchi yanasababishwa na ulipaji wa kodi kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, barabara, umeme na maji. Shigela amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanalipa kodi kwa hiari bila kusubiri kubugudhiwa na serikali, huku akieleza kuwa serikali itaendelea kupambana na wakwepa kodi wanaoingiza bidhaa za magendo nchini kwa kupitia bandari bubu zilizopo kandokando ya Bahari ya Hindi. “Nchi yoyote haiwezi kupiga hatua ya maendeleo bila wananchi wake kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa sababu kodi ndio kila kitu huwezi kujenga barabara kama wafanyabiashara hawataki kulipa kodi, huwezi kuimarisha huduma za afya kama hakuna kodi na pia huwezi kuimarisha mifumo ya elimu bila kodi,” alisema Shigela. Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Tanga, Specioza Owure amesema kuwa, maafisa hao wa TRA wanaofanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi, watafika maeneo mbalimbali yenye wafanyabiashara katika mkoa wa Tanga na watawaelimisha kuhusu umuhimu wa kodi na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. “Maafisa hawa wanatumia jitihada zote kuwaelimisha wafanyabiashara, tunafanya hivi ili kila mmoja afahamu wajibu wake wa kulipa kodi sambamba na kusogeza huduma za TRA karibu na wateja,” alisema Owure.Kampeni ya elimu kwa mlipakodi mkoani Tanga inatarajia kumalizika Juni 30, 2020 ambapo lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara, kusikiliza maoni na changamoto zao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha kulipa kodi kwa wakati. | 5 |
MAELFU ya watu waliojitokeza kushiriki kuaga na maziko ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba (49), yameelezwa kuwa ni kielelezo tosha cha matendo mema na ushuhuda wa maisha ya Ruge aliyoishi hapa duniani.Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Method Kilaini amesema maisha ya Ruge ni kielelezo kinachopaswa kuigwa na Watanzania hasa vijana katika kutenda mema na kuisaidia jamii.Askofu Kilaini alisema hayo jana katika viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba, wakati alipotoa heshima za mwisho kwa mwili wa Ruge Mutahaba, kabla ya maziko yaliyofanyika jana kijijini kwao Kiziru, nje kidogo ya mji wa Bukoba.“Tunapoomboleza leo, tunatiwa moyo na yale Ruge aliyoyafanya alipokuwa hai, nchi imempoteza kijana wa mfano na hazina ya kipekee, tutamkosa sana,” alisema Askofu Kilaini.Alisema ili kuenzi hazina kubwa na matendo mema aliyoyaishi, ni vizuri vijana kuishi kwa kufuata mema ya Ruge katika kufikia ndoto zao na kusaidia jamii zao kama alivyofanya.Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki, alisema katika kuenzi mazuri ya Ruge, ofisi yake itaendeleza na kukamilisha mipango yote iliyokuwa imebuniwa na Ruge katika eneo la uwekezaji nchini.Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media, Joseph Kusaga, alimuelezea Mutahaba kuwa ni mtu aliyekirimiwa vipawa vingi vya pekee na kujitoa kwa nguvu kubwa kusaidia na kuwainua wajasiriamali wadogo na vijana.Profesa Rwekaza Mukandala, Makamu Mkuu mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akitoa neno la shukrani, aliwashukuru wote, ikiwemo serikali, kanisa, marafiki wa ndani na nje ya nchi na wananchi wote kwa namna walivyojitoa kufanikisha maziko ya mtoto wao, Ruge.Katika hatua nyingine, msanii wa muziki nchini Mrisho Mpoto, alisababisha vilio alipokuwa akighani kuhusu namna Ruge alivyowasaidia watu wengi, akiwemo yeye mwenyewe kwa namna ya pekee. | 3 |
WAENDESHA bodaboda nchini wametakiwa kutochukua sheria mkononi inapotokea watu wamesababisha ajali wakiendesha barabarani.Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuf Masauni alisema hayo mjini hapa jana wakati akijibu swali la Nyongeza la Mbunge wa Kuteuliwa, Salma Kikwete (CCM). Salma alitaka kujua serikali inachukua hatua gani kuelimisha waendesha bodaboda ambao wamekuwa wakichukua hatua za papo kwa hapo na kupiga watu waliosababisha tatizo au ajali.Salma alisema pamoja na bodaboda kuleta faida nyingi zikiwemo ajira, usafiri na maendeleo, kumekuwa na changamoto za kuchukua hatua mikononi mara watu wanaposababisha ajali. Masauni alisema waendesha bodaboda hawatakiwi kuchukua hatua wanaposababisha vifo ili waepuke kuingia katika mkono wa sheria wakipelekwa mahakamani na kufungwa.Masauni pia alijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chwaka, Bhagwanji Maganlal Meisuria (CCM) aliyeuliza serikali ina mkakati gani kukomesha vitendo vya bodaboda kupora mali za abiria zikiwemo simu na mikoba ajalini.Masauni alisema waendesha pikipiki na bajaji wanaopora mikoba na simu za raia au abiria si wema bali wahalifu kama wahalifu wengine na hivyo Polisi wanatakiwa kuwashughulikia. Mbunge wa Musoma Mjini, Vedasto Manyinyi (CCM) alihoji lini serikali itatekeleza mkakati wa kupunguza tatizo la waendesha bodaboda kusababisha ajali za mara kwa mara na wizi. Masauni alisema vipo vyanzo vikuu vitatu vinavyosababisha ajali za barabarani nchini.Alivitaja vyanzo hivyo kuwa ni makosa ya binadamu ambayo huchangia kwa asilimia 76, ubovu wa magari asilimia 16 na mazingira ya barabara ambayo huchangia asilimia nane.Alisema makosa ya binadamu ni uendeshaji wa kizembe/ hatari, mwendo kasi, ulevi, uzembe wa wapanda pikipiki, wapanda baiskeli na watembea kwa miguu na sababu nyingine. Polisi inatoa elimu kwa waendesha boda namna nzuri ya utumiaji pikipiki ikiwemo kuvaa kofia ngumu, kukagua leseni kupunguza waendeshaji wasio na leseni wanaoweza kusababisha ajali. | 3 |
\
Na NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM
MAISHA ya duniani huwa ni ya muda na yanapotoweka matokeo yake mtu huzikwa kaburini.
Kiimani watu huamini kwamba mtu anapokufa na kuzikwa roho yake haizikwi bali mwili wake tu.
Ndio maana watu wengi walio hai wamejijengea utaratibu wa kufuata mila na desturi fulani ili kuwaheshimu na kudumisha uhusiano mzuri na roho za watu au ndugu zao waliowatoka.
Wengi wamejiwekea utaratibu wa kudhuru makaburi wakiamini kwa kufanya hivyo wanakutana na kuzungumza na ndugu zao kwani licha ya kutengana nao kimwili bado huendelea kuamini kwamba kiroho wako pamoja.
Pia wako watu ambao wamejiwekea utaratibu wa kutenga maeneo rasmi ya kifamilia ya kuwazika waliotutangulia na makabila mengi hufika makaburini mara moja au mbili kwa mwaka kuyafagilia na kufanya ibada na matambiko.
Hivyo, makaburi yanatakiwa kubaki mahali maalumu penye kustahili faragha na heshima yake.
Hata hivyo, kwa Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake maeneo ya kuzikia yamekuwa na changamoto nyingi.
Licha ya kuwapo kwa changamoto ya kujaa hasa katika maeneo maarufu ya kuzikia, changamoto nyingine ni kupotea kwa makaburi kutokana na sababu mbalimbali.
HALI HALISI VINGUNGUTI
Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, Kata ya Vingunguti ina watu 106,946.
Vingunguti ni kata ambayo ipo ndani ya Wilaya ya Ilala, Magharibi mwa Dar es Salaam.
Kwa muda mrefu ilizoeleka kuwa makaburi huweza kupotea kutokana na ama kuhamishwa kwa ajili ya kupisha shughuli zingine za kijamii kama ujenzi wa shule, hospitali au barabara lakini hili la Vingunguti linasikitisha.
Ukifika Vingunguti katika eneo la kuzikia lililoko Mtaa wa Miembeni jirani na Bonde la Butiama lazima utabaki na mshangao; kwamba unayoyaona ni makaburi au dampo la takataka.
Makaburi hayo sasa yanazidi kupotea na hata machache yaliyobaki nayo yako hatarini kutoweka.
Upande wa juu wa bonde hilo yanaonekana makaburi na katikati kuna njia inayolekea bondeni, lakini pembeni ya njia pia kuna makaburi ambayo yanaonekana yako nusunusu.
Kwamba zinaonekana alama tu zenye utambulisho wa marehemu husika (mawe na misalaba), lakini sehemu nyingine ya kaburi haionekani.
Mbaya zaidi katika eneo ambako sehemu ya makaburi imepotea pamegeuzwa dampo la kutupia takataka na hata alama chache zinazoonekana nazo ziko hatarini kupotea kabisa.
Hali hiyo inasababishwa na mmomonyoko wa udongo unaochochewa zaidi na mafuriko ya kila msimu wa mvua huku kukiwa hakuna hatua zinazochukuliwa.
Nyumba kadhaa zilizoko jirani na makaburi hayo nazo ziko hatarini kuanguka kutokana na mto kuzidi kusogelea katika upande wa makazi ya watu.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Miembeni, Salehe Kibavu anawatupia lawama wananchi waliogeuza eneo hilo kuwa dampo la taka na wakulima wa mbogamboga.
“Nasisi wananchi tunachangia uharibifu wa mazingira kwa sababu kama kule chini (bondeni) unaona wale (anamwonyesha mwandishi) wanalima mboga na wengine wanachimba mchanga, matokeo yake mvua zikinyesha maji yanapoteza mwelekeo mto unazidi kusogea katika makazi ya watu,” anasema Kibavu.
Anasema wamekuwa wakielimisha wananchi kuacha kuchimba mchanga na kutupa taka katika bonde hilo lakini matukio mengine yamekuwa yakifanyika nyakati za usiku.
WANANCHI
Wananchi wanaoishi karibu na eneo hilo wanasema kwamba kifo si mwisho wa maisha bali ni badiliko tu linalomwezesha mtu kuendelea na maisha mahali pengine hivyo ni vema makaburi hayo yakaheshimiwa.
“Yaani unaweza kupita hapa unakuta viungo vya watu vinazagaa na wakati wa mvua ukishuka huko chini unaweza kukutana na sanda au viungo vinasombwa na maji. Na hili tatizo si la leo tumeshalalamika mno.
“Wengi wetu tunaamini kwamba ndugu ama wazazi wetu walihama ulimwengu unaoonekana na kwenda ulimwengu usioonekana, yaani walihama ulimwengu wa wanadamu na kwenda ulimwengu wa roho ndio maana tumekuwa na utaratibu wa kuendelea kuwaheshimu.
“Kama mimi kila mwaka lazima niende nyumbani alikozikwa mama yangu kwa ajili ya kufanya dua ya kumwombea, huwa naenda kaburini kwake nasafisha kama msalaba umechakaa nabadilisha naweka mwingine,” anasema mkazi wa Miembeni, Salim Athumani (31).
Mkazi mwingine wa mtaa huo, Julieth Mwaipopo anasema maeneo ya makaburi yanapaswa kuheshimiwa na kuendelea kulindwa.
“Mbona yale ya Kinondoni wamejenga uzio au kwa sababu huku wanazikwa watu wa hali ya chini ndio maana wanayaacha?
“Mimi kwenye makaburi haya amezikwa dada yangu na kama kaburi halipo mimi naamini na yule mtu aliyezikwa pale hayupo, ni vibaya kwa sababu kama marehemu wakipuuzwa au kukasirishwa wanaweza kusababisha misiba, ugonjwa, umaskini na maafa mengine,” anasema Mwaipopo.
Mkazi mwingine wa mtaa huo Idrisa Mbakara, anaomba eneo hilo lilindwe ili kudhibiti utupaji taka.
“Yaani mimi naona kuliko kuzikwa hapa Dar ni afadhali ukazikwe nyumbani kwenu ulikozaliwa. Unaweza kushangaa makaburi yanahamishwa kwa shughuli zingine na mengine yamejaa lakini watu wanalazimisha kuzika,” anasema Mbaraka.
Naye Mbunge wa Segerea, Bonnah Kaluwa (CCM), ameomba jitihada za haraka zifanyike kunusuru makaburi hayo ili yasiendelee kupotea.
“Mimi binafsi eneo lenye makaburi naliheshimu mno tena naogopa hata kupita, hapa nimefika kwa taabu kwa sababu wananchi wangu wana tatizo. Makaburi yanazidi kupotea na hizi nyumba kama ikinyesha mvua kubwa zote zinaondoka yaani ni hatari tupu lakini bado watu wanaendelea kukaa,” anasema Kaluwa.
MANISPAA
Ofisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala, Tabu Shaibu anasema makaburi hayo si ya manispaa bali ni ya jamii hivyo yenyewe ndiyo inawajibika kuyatunza.
“Jamii kama kanisa au msikiti inaweza kuamua ikawa na eneo lake la kuzikia, sisi tunakuwa tunayatambua maeneo ya aina hiyo lakini jamii husika ndio inawajibika kuyatunza.
“Kuna makaburi mengine yako pale karibu na machinjio ya Vingunguti ni ya jamii lakini watu walipoanza kuyageuza dampo la takataka Waislamu walijitokeza na kujenga uzio, hivyo na hawa wa Miembeni wachukue tahadhari ili makaburi ya ndugu zao yasiendelee kupotea,” anasema Shaibu.
Kwa mujibu wa ofisa huyo kwa makaburi yaliyo chini ya jamii kibali cha kuzikia huwa kinatolewa hospitalini lakini kwa yale ya manispaa kibali hutolewa na wao.
“Makaburi kama yale yaliyoko Karume au Buguruni yako chini yetu ndiyo maana tunawajibika kuyatunza,” anasema.
Kuhusu nyumba hizo anasema eneo hilo tayari ni hatarishi lakini wakazi wengi wa mabondeni wamekuwa wakikaidi kuhama. | 3 |
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019 kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza. “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake. | 5 |
SERIKALI imeamua kusitisha mikataba ya wakandarasi wawili wa miradi ya maji kutokana na ucheleweshaji wa kazi uliokithiri.Akizungumza na vyombo vya habari jijini hapa jana, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa, alisema serikali imeamua kusitisha mikataba ya wakandarasi hao waliokuwa wakitekeleza miradi hiyo katika mikoa wa Lindi na Kigoma.“Serikali imesitisha mikataba kutokana na kuchelewesha kazi na hivyo kusababisha wananchi wa maeneo hayo kutopata huduma ya majisafi na salama kwa muda mrefu,” alisema Profesa Mbarawa.Profesa Mbarawa aliwataja makandarasi hao ni Overseas Infrastructure Alliance (India) Pvt. Ltd ya Mumbai nchini India, anayejenga mradi wa majisafi na usafi wa mazingira mjini Lindi na Spencer Services Ltd aliyekuwa anajenga mradi wa majisafi na usafi wa mazingira Kigoma.Alisema miradi hiyo imechukua muda mrefu kukamilika, mkandarasi wa Lindi alipaswa kukamilisha Machi 17, 2015 kwa mujibu wa mkataba wa awali, lakini aliongezewa muda hadi Desemba Mosi, 2015, hadi leo hajakamilisha na amefikia asilimia 92.3.Kwa upande wa mkandarasi wa mradi wa Kigoma, alipaswa kukamilisha kazi Machi 17, 2015, kwa mujibu wa mkataba wa awali, aliongezewa muda hadi Desemba 23, 2015 na hadi sasa hajakamilisha mradi huo ambao umefikia asilimia 87.Miradi yote miwili ilianza kutekelezwa mwaka 2013. Profesa Mbarawa alisema pamoja na kuwasimamisha kazi wakandarasi hao, serikali itaendelea kuwachukulia hatua nyingine za kinidhamu ili iwe fundisho kwa wakandarasi wengine wenye tabia kama hizo.Alisema baada ya kusitishwa mikataba hiyo, tayari wizara imechukua hatua za kutowapatia kazi nyingine yoyote wakandarasi hao. “Tayari tumeshaiandikia barua Benki ya India ya kuitaka iishikilie pia (dhamana) ijulikanayo kama Retention Money Bank Guarantee ya Kampuni ya Oversees Infrastructure Alliance iliyokuwa ikitekeleza mradi wa Lindi,” alisema.Kwa upande wa mkandarasi wa Kigoma, Spencon Services Ltd, tayari fedha ya udhamini wa ufanisi imeshaingia katika akaunti ya wizara yenye thamani ya Euro milioni 1.5.Aidha, timu ya wataalamu wanaendelea na uhakiki na kama kujitokeza madai mengine basi atakatwa kwenye hati yake ya mwisho ya madai. Alisema ili kufanya makabidhiano ya kazi na kampuni hizo ili ziondoke maeneo ya miradi, wizara imeunda timu itakayofanya kazi ya kuhakiki kazi zilizofanywa na zilizobakia kwa ajili ya kufanya makabidhiano ya kazi.Timu hizo tayari zimeshaanza kazi. “Baada ya kazi ya uhakiki kukamilisha mhandisi mshauri ataandaa mikataba kwa ajili ya kazi zilizosalia pamoja na makisio ya kazi zilizosalia,” alisema Profesa Mbarawa.Kwa upande wa mradi wa Lindi, wizara itamalizia kazi zilizobaki ikiwemo ya kununua gari la majitaka na mfumo wa kuendesha mitambo, na kwa Kigoma, itamalizia kazi zilizobaki ikiwemo ujenzi wa kitekeo cha maji. | 3 |
Derick Milton, Simiyu Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mtemi Andrew Chenge amekabidhi Kompyuta tano na Mashine ya kuchapisha kwa shule ya sekondari Simiyu iliyoko mjini Bariadi. Kompyuta hizo zimetolewa na mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF) kwa ajili ya kuunga mkono utekelezaji wa mkakati wa kufundisha wanafunzi kwa njia ya mtandao. Akikabidhi msaada huo mke wa mbunge huyo, Tina Chenge, mbele ya Mkuu wa Mkoa, Antony Mtaka amesema kuwa Kompyuta hizo zitasaidia kuinua kiwango cha elimu katika wilaya hiyo. Amesema kuwa mbunge huyo aliamua kutoa vifaa hivyo kwa shule hiyo ili kiwe kituo cha taaluma bora katika Mkoa wa Simiyu kwani kitasaidia kuboresha hali ya elimu mkoani humo pamoja na shule yenyewe. Akipokea vifaa hivyo Mtaka, amemshukuru mbunge kwa msaada huo, n na kusema msaada huo utasaidia utekelezaji wa mpango mkakati mpya wa kufundisha watoto kwa anjia ya mtandao. ” Katika kipindi hiki ambacho shule zimefungwa kutokana na janga la corona, tumezindua mkakati huu ili wanafunzi wafundishwe kwa njia ya mtadao na msaada huu umekuja wakati muafaka,” amesema Mtaka. Naye Mkuu wa shule hiyo, Paul Susu amemshukuru Chenge kwa msaa huo, ambao utasaidia kuendeleza jitihada walizoanza za kufundisha kwa njia ya mtandao. | 3 |
THERESIA GASPER-GASPER-DAR ES SALAAM BAADA ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania,
Kocha Msaidizi wa Azam, Iddy Nassor ‘Cheche’,
ameitaka Simba ijiandae kukutana
na maumivu na kipigo kutoka kwao. Azam na Simba zitashuka dimbani kuumana, katika pambao la
Ligi Kuu Tanzania Bara, litakalopigwa Marchi 4 mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam. Kauli ya kishujaa ya Cheche imekuja siku moja baada ya
kikosi chake kuibuka na ushindi huo dhidi ya JKT Tanzania, mchezo uliochezwa
Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. Akizungumza na MTANZANIA jana, Cheche alisema haikuwa
kazi rahisi kwao kupata pointi tatu ugenini, lakini kutokata tamaa kwa
wachezaji wake na kupambana dakika zote tisini kumewasaidia waweze kutoka kifua
mbele. “Kwa sasa tunarejea nyumbani kujiandaa na mchezo
unaofauata dhidi ya Simba, kwani mtoto atakuwa hatumwi dukani hivyo
tutahakikisha hatuwapi tena nafasi Simba ya kutufunga kirahisi,” alisema. Alisema katika mchezo dhidi ya JKT Tanzania, kuna baadhi
ya makosa aliyabaini ambayo ataendelea kuyatafutia tiba ili yasijitokeze kwa
mara nyingine. Cheche alisema wataendelea kupambana na kutoruhusu makosa
kama ilivyokuwa kwenye mechi za nyuma ambako walipata sare na kufungwa. Alisema kwa sasa wanatizamia nafasi za juu zaidi kwenye
msimamo wa ligi hivyo usipokuwa makini unaweza ukapoteza na kushuka chini. | 4 |
Na TUNU NASSOR -DAR ES SALAAM SUALA la Meya wa Ubungo, Boniface Jacob na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, limechukua sura mpya baada ya meya huyo kuitwa Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma na kutakiwa kujibu shauri lililofunguliwa la matumizi ya ofisi ya umma kwa shughuli za chama chake. Machi 22, mwaka huu Meya Jacob aliwasilisha mashitaka dhidi ya Makonda kwa Sekretarieti hiyo, akitaka achukuliwe hatua za nidhamu kwa kukiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kutumia vyeti feki na hivyo kukosa sifa ya kuwa kiongozi. Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutoka katika mahojiano na sekretarieti hiyo jana, Jacob alisema sekretarieti hiyo imemwomba kujibu shauri hilo ikisema kwa kuwa hata yeye aliwahi kutumia Ofisi za Manispaa ya Ubungo kwa vikao vya chama chake. “Wameniomba kuondoa shauri hili kwa madai kuwa walipomwita Makonda alisema tuyamalize kwa kuwa hata mimi nilitumia ofisi ya umma kufanya vikao vya chama… mimi nimesema ruksa kunihukumu kama wana ushahidi wa kutosha,” alisema Jacob. Alisema uhalali wa Makonda kumhoji kuhusu kufanya vikao vya chama katika ofisi ua umma ndiyo mwanzo wa uhalali wa kumhoji mkuu wa nchi uhalali wa kufanya vikao vya chama Ikulu. “Hakuna kikao ambacho nilikiongoza mimi nikiwa na wafuasi wa chama, ninachojua nilitembelewa na Frederick Sumaye. Kiongozi wa Chadema akinitembelea nimkatae? “Lakini wenzetu wamefika mbali kwa kuvaa sare za chama na kuzungumza masuala ya chama,” alisema. Alisema wanaporuhusu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kumuuliza kuhusu hilo walipaswa waanze kujitafakari kuwa kuna Halmashauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inafanyika Ikulu. Alisema walimwambia hakuna mtu aliyewahi kulalamika kwa nini mikutano ya CCM inafanyika Ikulu. “Sheria inasema wao waliposikia tu kuwa Makonda ana vyeti feki walitakiwa kumwita na si kusubiri mtu aende kushtaki. “Wao kama wasimamizi wa maadili ya umma wakiona mtu anarudisha fedha za rushwa benki hawakustahili kusubiri mtu wa Chadema kwenda kushtaki,” alisema Jacob. Jacob alisema alipewa dakika 10 za kuandika malalamiko kwa nini CCM inafanyia vikao vyake Ikulu. “Nimewakabidhi ushahidi wa picha na video za vikao vya Chama cha Mapinduzi Ikulu,” alisema Jacob. Alisema lengo lake si kulalamika kuwa CCM inafanyia vikao vyake ikulu bali suala la vyeti feki ambalo anahitaji lifikishwe katika Baraza la Maadili. | 3 |
BAADA ya kutoka suluhu katika mechi ya kwan- za ya mtoano kati ya Pamba na Kagera Sugar, makocha wa timu hizo wamesema wanajipanga kumaliza mechi mwis- honi mwa wiki iliyopita.Pamba ilicheza na Kagera kwenye uwanja wa Nyamagana mjini hapa juzi na kutoka suluhu na hivyo kujiweka kwenye mazin- gira magumu katika mechi ya marudiano itakayo- chezwa Kagera mwishoni mwa wiki hii ambapo timu itakayoshinda itacheza Ligi Kuu msimu ujao.Akizungumzia mechi hiyo kocha wa Kagera, Mecky Maxime alisema walishindwa kumaliza mechi ugenini lakini wana- jipanga kuimaliza nyum- bani.“Tunajipanga kwa me- chi ya marudiano nyum- bani ili tupate matokeo mazuri maana hapa (Nya- magana) tumeshindwa kuimaliza.”Naye kocha wa Pamba, Ally Kisaka alisema licha ya sare hiyo timu yake itapambana kupata ushindi katika mechi ya maru- diano.Kisaka aliwaomba wadau na wapenzi wa soka mkoani Mwanza wasikate tamaa, bali waendelee kusapoti timu yao ili ivuke hatua hiyo na kucheza Ligi Kuu.Kocha huyo wa zamani wa Zanzibar Heroes ali- wapongeza wachezaji wake kwa kufuata maelekezo yake muda wote. | 4 |
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amesema mchango wa sekta ya utalii katika Pato la Taifa kwa sasa ni zaidi ya asilimia 17 na inaongoza katika kuliingizia Taifa fedha za kigeni, ikichangia takribani asilimia 25.Akiwasilisha bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2015/16 jana bungeni, Nyalandu alisema mwaka 2014, idadi ya watalii waliongia nchini ilikuwa 1,140,156 ikilinganishwa na 1,095,884 mwaka 2013.“Watalii hao walitembelea vivutio mbalimbali nchini na kuliingizia Taifa Dola za Kimarekani bilioni 1.9 ikilinganishwa na 1.8 zilizopatikana mwaka 2013,” alisema Nyalandu.Hata hivyo, alisema Wizara inakabiliwa na changamoto mbalimbali alizozitaja kuwa ni ujangili na biashara haramu ya nyara; migogoro ya mipaka na uvamizi wa maeneo ya hifadhi na ukwepaji ulipaji tozo za utalii.Nyingine ni ubovu wa miundombinu, mwamko mdogo wa Watanzania kutembelea vivutio vya utalii.“Kutokana na tishio la ugaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki pamoja na mlipuko wa ugonjwa wa ebola, baadhi ya wageni waliahirisha safari za utalii,” alisema.Alisema katika kukabili changamoto hizo, Wizara imejipanga kushirikisha wadau mbalimbali katika uhifadhi na matumizi endelevu ya maliasili, malikale na shughuli za utalii.Kuhusu uhifadhi na usimamizi wa wanyamapori, alisema zilijumuisha kuendesha siku za doria 103,895 ndani na nje ya Mapori ya Akiba. Alisema katika doria hizo, watuhumiwa 1,082 walikamatwa na jumla ya kesi 998 zilifunguliwa katika Mahakama mbalimbali nchini.“Kesi 424 zenye watuhumiwa 259 zilimalizika kwa wahalifu kulipa faini ya Shilingi 268,250,000 na wengine 18 kufungwa jela jumla ya miezi 26. Kesi 256 zenye watuhumiwa 614 zinaendelea katika mahakama mbalimbali,” alifafanua Nyalandu.Alisema nyara za serikali zilizokamatwa ni nyamapori yenye kilo 9,658.5, meno ya tembo 182 yenye uzito wa kilo 256, kucha za simba 451, meno ya simba 65, ngozi 60 za wanyamapori mbalimbali, ndege hai 65, kenge 149, lita za mafuta ya simba na matenga 50 ya samaki.“Mifugo na mali nyingine zilizokamatwa ni pamoja na ng’ombe 17,489, mbao 1,828, magogo 130 na magunia ya mkaa 915. Aidha, silaha 132 za aina mbalimbali zilikamatwa na kati ya hizo, bunduki 84 ni za kivita,” alieleza.Kuhusu ulinzi wa maisha ya wananchi na mali zao dhidi ya wanyamapori, alisema Wizara ilipokea taarifa za kuuawa kwa wananchi 42 katika wilaya za Kilwa, Tunduru, Tabora na Ilemela.Alisema Sh 36,300,000 zililipwa kama kifuta machozi kwa ajili ya wananchi 45 waliopoteza maisha na waliojeruhiwa katika wilaya za Singida, Ngorongoro, Masasi, Serengeti, Tarime, Mpanda, Tabora, Tunduru na Ilemela.Aidha, alisema Juni Mosi, mwaka huu, Wizara itatangaza matokeo rasmi ya sensa iliyofanywa ya wanyamapori katika mifumo ya ikolojia. | 5 |
['Real Madrid itataka kumsaini kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen mwezi Januari.(Marca)', 'Real Madrid pia wanaisaka saini ya mshambuliaji wa Red Bull Salzburg, 19 raia wa Norway Erling Haaland, ambaye amehusishwa na uhamisho wa kuelekea Manchester United. (AS)', 'Beki wa kulia wa Tottenham na Ivory Coast Serge Aurier, 26, amefichua kwamba alitaka kuondoka mjini London mwisho wa msimu uliopita na amekiri kwamba hajui hatma yake iko vipi katika klabu hiyo. (Football.London)', 'Aston Villa imehusishwa na kiungo wa kati wa Tottenham na Uingereza Eric Dier, 25. (Birmingham Mail)', 'Kazi ya Unai Emery kama mkufunzi Arsenal huenda ipo hatarani iwapo kikosi chake kitashindwa kufuzu katika kombe la klabu bingwa Ulaya msimu huu . (Times - subscription required)', 'Mchezaji wa zamani wa Uingereza na nahodha David Beckham anamlenga mshambuliaji wa Paris St-Germain na Ufaransa Kylian Mbappe, 20, kama mteja wake wa kwanza katika kazi yake mpya kama ajenti . (Mail)', 'Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya Man United Mark Robins amesema kwamba ilikuwa rahisi kwake kukataa kuwa mkufunzi wa Sunderland na kuamua kutia saini kandarasi mpya na klabu ya Coventry. (talksport)', 'Ajenti mmoja raia wa Urusi anadai kwamba aliiomba klabu ya Zenit St - Petersburg kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexander Lacazette ambaye alikuwa anagharimu £61m . (mirror) ', 'Kiungo wa kati wa Ufaransa na Man United Paul Pogba ,26, anakaribia kupona jeraha tayari kucheza mechi dhidi ya Liverpool mnamo tarehe 20 mwezi Oktoba licha ya ripoti ya kuvunjika kidole. (sun) ', 'Man United inaweza kutarajia ufadhili wa shati utaokagharimu £450m huku wakisaka kandarasi mpya.(ESPN)', 'Kiungo wa kati wa Newcastle na Uingereza Matty Longstaff , aliyefunga bao la ushindi katika mechi yake ya kwanza dhidi ya Man United mwezi huu , kwa sasa analipwa £850 kwa wiki na klabu hiyo. (sun) ', 'Kiungo wa kati wa Wolves na Ureno Jaoa Moutinho 33 anatarajiwa kukubali kuweka kandarasi mpya katika uwanja wa Molineux. (Birmingham Mail)', 'Wolves ina mpango wa kuimarika katikati ya safu ya ulinzi pamoja na safu ya katikati wakati wa dirisha la uhamisho la mwezi Januari (The Athletic, via Inside Futbol)', 'Mkufunzi wa zamani wa Arsenal Arsene Wenger amemwambia Aliyekuwa mshambuliaji wa Sunderland Kevin Phillips kwamba heri anemsajili yeye badala ya Francis Jeffers. (Mirror)', 'Kiungo wa zamani wa Man United Marouane Fellaini, 31 raia wa Ubelgiji ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya China ya Shandong Luneng, anasema kwamba Jose Mourinho hakupewa muda wa kutosha katika uwanja wa Old Trafford. (Mail)'] | 4 |
Katika mchezo wa kwanza, Yanga wakiwa nyumbani walipata ushindi mwembamba wa bao 1-0, hivyo katika mchezo huo wawakilishi hao wa Tanzania Bara, wanahitaji sare au ushindi wa namna yoyote ili kusonga mbele hatua inayofuata.Akizungumza na gazeti hili kabla ya timu kuondoka, msemaji wa Yanga Dismas Ten, alisema wamekwenda Shelisheli wakiwa na uhakika na ushindi kutokana na maandalizi mazuri ambayo wameyafanya tangu mchezo wao wa mwisho wa ligi dhidi ya Majimaji.“Timu imefanya mazoezi ya kutosha na kocha ameridhishwa nayo, lakini pia wachezaji wote wapo fiti kiafya na kiakili kwa ajili ya pambano hilo hivyo tunakwenda kwa ajili ya kupambana na kupata ushindi ambao utatuvusha raundi ya kwanza ya michuano hiyo ya Afrika,” alisema Ten.Msemaji huyo alisema katika mchezo huo watamkosa mshambuliaji wao Obrey Chirwa, kutokana na kukabiliwa na maumivu ya misuli ya paja aliyoyapata kwenye mchezo wa ligi uliopita dhidi ya Majimaji siku chache zilizopita.Ten alisema wanakwenda wakijua ubora wa wapinzani wao St Louis, na kocha wao George Lwandamina anatambua mbinu mbadala ambazo zitawasaidia kuhakikisha wanaibuka na ushindi wakiwa ugenini.Nyota 20 ambao wameondoka na kikosi cha Yanga jana asubuhi kwa Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya wakipitia Nairobi, Kenya na baadaye Shelisheli, ni Ramadhani Kabwili, Beno Kakolanya, Gadiel Michael, Juma Abduli, Hassan Ramadhani, Said Makapu, Geofrey Mwashiuya, Rafael Daud, Kelvin Yondani na Pius Buswita.Wengine ni Emmanuel Martin, Said Mussa, Ibrahim Ajibu, Youth Rostand, Patto Ngonyani, Nadir Haroub, Andrew Vicent, Papy Tshishimbi, Amiss Tambwe na Buruan Akilimali. | 4 |
RAIS mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Kikwete ambaye ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amewataka wahitimu wa shahada za ualimu, kujiandaa kisaikolojia kufundisha shule za msingi, badala ya sekondari kama walivyotarajia.Alisema hayo juzi kwenye mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam cha Elimu Mkwawa (MUCE), Iringa baada ya kuwatunuku wahitimu shahada.Alisema, serikali hivi sasa inawapeleka walimu waliohitimu shahada za ualimu, kufundisha shule za msingi, jambo ambalo halikupokelewa vyema na walimu, wakidai kushushwa hadhi, kwa kuwa waliamini stahili yao ni sekondari. Tunaungana na wadau wa elimu, kumpongeza Dk Kikwete kwa kuwaasa walimu kujiandaa kufundisha shule za msingi, kwani mwelekeo wa serikali sasa ni mapinduzi ya viwanda na mapinduzi ya elimu.Ni matarajio yetu walimu waliohitimu juzi na waliohitimu zamani, sasa wameelewa vyema nia ya Serikali ya Awamu ya Tano kuboresha elimu ya msingi na kujenga msingi bora wa elimu ya juu. Ni vizuri wakauelewa na pia kuupokea vyema mpango huo wa serikali, unaolenga kuboresha elimu ya msingi na pia kuwahakikishia ajira kubwa wahitimu wa ualimu kutokana na shule za msingi, kuhitaji walimu zaidi wenye shahada.Kwa wasioelewa maana ya mpango huo ni vyema wakarejea kauli ya Rais mstaafu Kikwete kuhusu mabadiliko, ambayo mfumo wa elimu nchini umepitia tangu ukoloni hadi leo. Kimsingi, mpango huo umelenga kuboresha utoaji wa elimu ya msingi ili kwenda na wakati, teknolojia na utandawazi kuziba pia ombwe la walimu wa darasa la saba (UPE), kidato cha nne (Daraja C) na wa diploma walioostaafu au kufa.Kwa kuwa elimu yetu inapita katika vipindi na mfumo tofauti, ni vizuri wahitimu wa ualimu wakaelewa mantiki ya serikali kuamua walimu wenye shahada, wakafundishe shule za msingi ili kuboresha taaluma ili tushindane na nchi za nje. Wazazi, walimu, wadau wa elimu na wanafunzi ni mashahidi wa malalamiko kuhusu ubora wa elimu inayotolewa, kufuatia baadhi ya wahitimu kutokidhi matarajio ya viwango vya waajiri. Malalamiko hayo yakiwemo ya wahitimu shule za msingi kutojua vyema Kiingereza, yanaelekea kupata jibu sahihi, kwa hatua hizi za serikali kwa kuboresha sifa za walimu watakaofundisha.Ni muhimu basi kama Taifa, kila mmoja kwa nafasi yake, ashiriki mageuzi haya ya elimu kwa kushirikiana na serikali kuboresha mfumo mzima wa utoaji elimu ili ukidhi mahitaji ya soko. Serikali inatekeleza sera ya viwanda, ambayo inahitaji wasomi wenye weledi wa kuendesha viwanda na kufanya biashara. Hivyo, ni muhimu kwa vyuo vye elimu kubadili mitaala, kukidhi utoaji elimu bora, utakaokidhi matarajio hayo. | 3 |
NAIROBI, KENYA KINARA mwenza wa muungano wa upinzani wa NASA Kalonzo Musyoka, ameyashambulia mataifa ya magharibi hasa Marekani ambayo alisema inasambaratika na hivyo haina uwezo wa kuisaidia Kenya. Akizungumza pamoja na vinara wenzake wa muungano huo kwenye Bustani ya Uhuru mjini hapa juzi, Kalonzo alisema Kenya haihitaji msaada wa mabalozi wa mataifa ya magharibi na kwamba mpango wake na Raila Odinga kuapishwa uko palepale. Kiongozi huyo wa Chama cha Wiper, alimlaumu Balozi wa Marekani Robert Godec kwa kile alichosema kupenda kuingilia masuala ya Kenya ilihali kwao (Marekani) kuna waka moto. “Balozi wa Marekani anapaswa kuisaidia nchi yake ambayo kwa sasa inachukuliwa kuwa imesambaratika. Wamarekani wanaandamana kila siku kwa sababu hawana imani na uongozi. Watu kote duniani wanalilia uhuru, ukweli na haki hali ambayo haina tofauti na hapa Kenya,” alisema. Musyoka pia alisisitiza kuwa yeye na Odinga walishinda Uchaguzi Mkuu wa Agosti 8 2017 lakini wakaibiwa kura. “Tulishinda uchaguzi huo peupe lakini Mahakama ya Juu ilipoamuru Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ifungue kanza data, Jubilee iliwatisha wakakataa kufungua. Kama wanaamini hatujashinda, basi waagize kanza data zifunguliwe ili ulimwengu ujue ni nani msema kweli,” akasema. Wakizungumza wakati wa mkutano wa Bunge la Wananchi katika bustani hiyo, Odinga alisema viongozi wa Jubilee wanarudisha Wakenya siku za giza kwa kutaka kuongoza wao na kubadilisha katiba. Alimshambulia Kenyatta kwa hatua yake ya kuteua wakuu wa polisi akisema hiyo kinyume cha sheria. “Wakenya wanapaswa kuwakataa Uhuru na Ruto na wapinge mipango yao ya kutaka kuturudisha siku za nyuma. Sisi tunaenda Kanaani nao wanataka kuturudisha Misri.” Odinga alisema NASA itafanya mikutano Suswa eneo la Narok, Migori na Kisii kabla ya kuelekea Nairobi katika sherehe ya kuapishwa kwake. Kalonzo pia aliishambulia Jubilee kwa kishindwa kutimiza ahadi zake, ikiwemo elimu ya bure ya sekondari. “Waliiga mipango yetu ambayo ilikuwa tumeipanga vilivyo na sasa wameshindwa kuitekeleza. Mmeona elimu ya bure nyinyi?” akauliza. | 2 |
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda ameutaka uongozi wa Kiwanda cha Kutengeneza Magunia ya Mkonge cha TPM (1998 LTD ) mkoani Morogoro, kutotekeleza mpango wake wa kusitisha uzalishaji kutokana na ukosefu wa soko la bidhaa zao, kwa kuwa tayari serikali imeshaanza kuzitatua changamoto hizo.Waziri Kakunda amesema hayo juzi mjini Morogoro baada ya kukutana na uongozi wa kiwanda hicho na kusomewa taarifa na Maneja Mwandamizi wa MeTL anayeshughulikia uzalishaji wa magunia pamoja na mashamba ya Mkonge, Ndekirwa Nnyari, kuhusu changamoto za muda mrefu zinazokikabili kiwanda hicho.Kakunda amesema serikali inathamini mitaji inayowekezwa na wawekezaji katika viwanda na pia ina jukumu la kulinda mitaji yao isipote bure, kuwalinda watu wanaozalisha ajira zinazowanufaisha Watanzania wengi pamoja na kuiingizia mapato serikali.“Uongozi wa kiwanda andikeni barua niipate Jumatatu (leo) ikielezea changamoto zilizopo, maandiko haya yaandikwe kitaalamu,” amesema.Baada ya kufikishwa kwake atakutana na kamati ya uchumi na fedha ya Baraza la Mawaziri iweze kuona ni namna gani ya kusaidia kuzitatua changamoto za muda mrefu ikiwemo ya uingizwaji wa magunia ya jute kutoka nchi za barani Asia na kuuzwa kwa bei ya chini.Waziri Kakunda amesema yapo mahitaji makubwa ya ndani ya magunia kwa kiwango cha zaidi ya milioni 20 na kuutaka uongozi wa kiwanda hicho kuongeza uzalishaji mkubwa kwani uwezo wa kiwanda hicho ni kuzalisha magunia milioni 10 kwa mwaka. | 5 |
Lechantre raia wa Ufaransa alisema kuwa alipomuona Mkude ameumia akilalamika na kuwahishwa hospitali alianza kukuna kichwa juu ya majaliwa ya timu hiyo kwenye eneo la kiungo kuelekea katika michezo iliyosalia.“Haikuwa kitu rahisi kukishuhudia, Mkude ni moja ya wachezaji muhimu hapa kikosini, anacheza vizuri eneo la kiungo hivyo kuumia kwake ilinishtua kuelekea katika mechi zilizosalia lakini afadhali sasa anaendelea vizuri na ataungana nasi mazoezini muda si mrefu,” alisema Lechantre.Mkude alipata majeraha ya kifundo cha mguu juzi baada ya kugongana na Mzamiru Yassin wakiwa mazoezini ambapo kutokana na majeraha hayo ilibidi awahishwe hospitali.“Wachezaji wengine nao kina Mbonde (Salim) na Niyonzima (Haruna) nao wanaendelea vizuri, wamekuwa wakikimbia wenyewe wakiendelea na programu zao lakini nimepewa taarifa na daktari kuwa baada ya kama wiki moja watakuwa tayari kuungana na wenzao katika mazoezi ya kitimu,” alisema Lechantre.Simba inajiandaa na mchezo wake wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Njombe Mji utakaopigwa Njombe Aprili 3, mwaka huu inaendelea na mazoezi yake kwenye Uwanja wa Boko, Dar es Salaam. | 4 |
Na Aziza Masoud,
HIMOFILIA ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda ambao unasababishwa ukosefu wa kiwango cha kutosha cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu na kusababisha damu kuvuja kwa muda mrefu.
Ugonjwa huu ambao asilimia 30 ya wagonjwa huzaliwa nao kutokana na mabadiliko ya vinasaba pia hurithiwa na huwakumba jinsia zote.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Damu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk Stella Rwezaura anaeleza kuwa asilimia 97 ya wagonjwa wa himofilia hawajui kama wanaougonjwa huo na hawajawahi kupatiwa vipimo vyovyote ili kujua hali ya ugonjwa.
Anasema mtu mwenye ugonjwa huu ataishi nao kwa maisha yake yote bila kupona lakini una uwezo wa kutibika.
Aina za Himofilia
Anasema kuna aina mbili za himofilia ikiwemo wagonjwa wengi kupata himofilia A,mara nyingi wagonjwa wa kundi hili hawana chembechembe za kugandisha damu . Anabainisha kundi lingine ni Hemofilia B,mara nyingi huwapata wagonjwa wachache wenye upungufu wa chembechembe namba 9.
“Kwa pamoja makundi hayo yote mawili ya Hemofilia A na B wote kwa pamoja huvuja damu kwa muda mrefu kuliko wagonjwa wa kawaida,”anasema Dk.Stella.
Anasema mgonjwa wa himofilia kwakuwa anakuwa anavuja damu katika viungo inamfanya anakosa nguvu na kushindwa kufanya shughuli zake za kila siku.
Dalili za himofilia
Anabainisha dalili za Ugonjwa huo zinazoonekana kwa macho ni pamoja na kutokwa damu mfululizo kwa muda mrefu unapotokea mchubuko, kukatwa au kujikata, kutoneshwa ama jitonesha kidonda .
Itaendelea wiki ijayo
Makala haya yameandaliwa kwa msaada wa Chama Cha Madaktari wa Himofilia Tanzania . | 0 |
Hata hivyo, mamlaka hiyo imeonya kuwa bei hiyo ya mafuta nchini haitaweza kupungua kwa kiasi kikubwa, kutokana na kushuka kwa thamani ya Shilingi dhidi ya dola ya Marekani pamoja na kutokubadilika kwa ushuru mbalimbali wa ndani wa mafuta.Pamoja na hayo, Kampuni ya Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PICL) imeiomba Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Nishati na Madini kuingilia kati na kuihamasisha Serikali iongeze ulinzi katika mabomba na matangi ya mafuta Kurasini, ambayo kwa sasa hayako salama na ni hatari kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.Akiwasilisha taarifa ya ukokotoaji wa mafuta kwa kamati hiyo Dar es Salaam jana, Mtaalamu kutoka EWURA, Lorivii Long’idu, alikiri kuwa ni kweli kwa sasa bei ya mafuta katika soko la dunia imekuwa ikishuka kwa kasi ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.“Bei hizi zimeshuka kutoka dola 100 hadi kufikia dola 60 kwa pipa ambayo ni sawa na asilimia 40 kutokana na kudorora kwa uchumi wa bara la Ulaya katika kipindi hiki na kuwepo kwa tofauti za mitazamo ya kisiasa hasa katika nchi za Marekani na Urusi,” alisema Long’idu.Hata hivyo, alisema pamoja na bei hizo kushuka tangu Julai hadi Desemba mwaka jana, kwa kawaida kwa Tanzania huchukua takribani miezi miwili bei hiyo kuweza kufikia soko la ndani.Alisema bei zote za mafuta katika soko la ndani, zimekuwa zikishuka kuanzia robo ya mwisho wa mwaka jana sambamba na kushuka katika soko la dunia na kwamba bei hizo hukokotolewa na Ewura kwa kutumia kanuni maalum, inayotumia gharama halisi za uagizaji mafuta nchini, zinazotokana na meli za mafuta yaliyopokelewa mwezi husika yaliyonunuliwa mwezi wa nyuma yake.Alisema uhusiano wa bei za soko la dunia na soko la ndani, unapishana kwa miezi miwili na kwamba mafuta yanayotumika mwezi huu, Ewura ilikokotoa bei zake tangu Novemba kulingana na bei ya mafuta yaliyonunuliwa katika soko la dunia mwezi huo.Long’idu alisema kwa hali ilivyo sasa bei za mafuta ghafi katika soko la dunia, zitaendelea kushuka kama hakutakuwa na tukio lisilo la kawaida duniani, hali itakayochangia kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo katika soko la ndani japo si kwa kiwango sawia.Alisema pamoja na bei kushuka katika soko la dunia kwa kiwango chochote kile, bei ya ndani itashuka kulingana na thamani ya Shilingi dhidi ya dola ya Marekani lakini pia ushuru uliopo ambao katika petroli unatozwa Sh 878, dizeli Sh 754 na mafuta ya taa Sh 701 kwa lita ambao wenyewe haubadiliki.Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Nishati na Madini, Jerome Bwanausi, aliagiza Ewura na PICL wanapokokotoa bei za mafuta kuhakikisha wanatoa ufafanuzi wa hali halisi ya bei za soko la dunia na utaratibu mzima wa uingizaji wa mafuta nchini ili kuondoa habari potofu zinazosambazwa juu ya bei hizo za mafuta.Aidha, aliagiza Wizara ya Nishati na Madini kuchukua hatua za haraka na kushughulikia suala la ulinzi katika mabomba na matangi ya mafuta ili kudhibiti hali ya hatari ya kulipuliwa kwa matangi hayo na kuhatarisha usalama wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.“Hii ni hatari sana kwa namna yale mabomba yalivyo hayana ulinzi, watu wanatoboa mabomba na kuiba mafuta na kuweka maboya, endapo mtu yeyote akitupa moto pale Dar es Salaam nzima itakuwa haipo, hatua za haraka zichukuliwe, na kamati ipatiwe taarifa za ulinzi wa sasa katika eneo hilo,” alisisitiza.Aidha, alisema kutokana na hali ya hatari ya usafirishaji wa mafuta iliyopo sasa kupitia malori hasa katika vijiji malori hayo yanakopita na kulala, ni vyema Serikali ikaanza mchakato wa kuchimba mabomba ya kusafirishia mafuta na kufufua reli ili kudhibiti usalama wa wananchi. | 5 |
KLABU ya Manispaa ya Kinondoni (KMC) imeweka wazi suala la kuwapa wachezaji wake mikataba wa mwaka mmoja mmoja.Akizungumza na gazeti hili Meneja wa Klabu hiyo, Walter Harrison alisema, “Mkataba wa mwaka mmoja unamfanya mchezaji ajitume ili kujihakikishia kuongezewa mkataba kwa msimu mwingine.Mara nyingi mchezaji akipewa mkataba wa miaka mingi hubweteka.’’ Harrison alisema pia kuna wachezaji wa kikosi cha vijana chini ya miaka 20, hao watapewa mikataba ya muda mrefu, kuanzia miaka miwili na kuendelea.KMC iliyopanda daraja msimu huu imesajili wachezaji ishirini na sita kwa ajili ya kujiandaa na msimu wa ligi kuu 2018/2019. Miongoni mwa wachezaji hao ni pamoja na mlinda lango wa zamani wa Simba, Juma kaseja, huku wakiacha nafasi nne kwa ajili ya dirisha dogo.Pia wameendelea kuthamini mchango wa wachezaji walioipandisha daraja kwa kuwaongezea mkataba wa mwaka mmoja miongoni mwa wachezaji hao ni Abdulhalim Humoud, Ally Ramadhani, Rehani Kibingu na Rayman Mgungila.Kikosi hicho kitaanza kambi mwishoni mwa wiki ijayo na tayari wameshatoa taarifa kwa wachezaji juu ya siku rasmi ya kuripoti kambini. | 4 |
NEW YORK, MAREKANI RAIS wa Marekani, Donald Trump, amedaiwa kuwashutumu wahamiaji wanaoingia nchini humo kutoka Haiti, El Salvador na Bara la Afrika kwa kuwafananisha na uchafu kwa madai wanaharibu nchi hiyo hivyo wanapaswa kuzuiliwa. Kwa mujibu wa gazeti la The Washington Post, limesema Trump alizungumza hayo juzi wakati alipokutana na Kamati ya Bunge katika majadiliano yao Ikulu na kuhoji ni kwanini Marekani inapokea wahamiaji kutoka nchi hizo badala ya nchi kama Norway. “Wanasiasa fulani wa Washington hupendelea kupigania mataifa ya kigeni, lakini Rais Trump atawapigania raia wa Marekani pekee. Kama mataifa mengine ambayo yana wahamiaji wanaofaa kuwa nchini humo, Rais Trump anapigania suluhisho la kudumu linalofanya taifa hilo kuwa thabiti kwa kuwakaribisha wale ambao wana mchango katika jamii, hukuza uchumi wetu na kuingiliana na raia wa taifa letu,” ilisema taarifa ya Msemaji wa Ikulu, Raj Sha. Aidha, kauli ya Trump ilidhihirisha kikwazo cha kupokea mamia ya wahamiaji pamoja na kuvurugwa mapendekezo ya maseneta 6 wa vyama vya Republican na Democrat ya kupokea wahamiaji zaidi kutoka mataifa ya kigeni. Trump alithibitisha kuwa kamwe hatakubali mkakati wa muda mfupi ambao ni dhaifu na hatari kwani unahatarisha maisha ya raia wa Marekani, mbali na kutowaruhusu wahamiaji wanaotaka maisha mazuri wakiwa ugenini ijapokuwa kwa kupitia njia halali. Seneta wa Democrat, Richard Durbin, alikuwa akizungumza kuhusu vibali vya muda wa kuishi vinavyotolewa kwa raia wanaotoka katika mataifa yaliyokumbwa na majanga, vita ama milipuko ya magonjwa. Mtandao wa Shirika la habari la CBS la nchini humo, ulisema Trump aliwaambia wabunge kwamba Serikali badala yake inachukua wahamiaji kutoka Norway, ambayo waziri wake mkuu, Erna Solberg, alimtembelea rais huyo katikati ya wiki hii. Seneta Lindsey Graham, ambaye ni mwanachama wa chama cha Republican kutoka Jimbo la Carolina Kusini, pia alihudhuria mkutano huo lakini hakuweza kuzungumzia kuhusu matusi hayo yaliyotolewa na Rais Trump. Miaka mitatu iliyopita gazeti la New York Times liliripoti kwamba, Trump alidai kuwa raia wa Haiti wote wana “Ukimwi” wakati wa mkutano kuhusu wahamiaji. Mbunge wa Jimbo la Maryland kupitia chama cha Democrat, Elijah Cummings, amechapisha ujumbe katika mtandao wa Twitter akisema: “Nayashutumu matamshi hayo yasiyosameheka na yanayoshusha hadhi ya ofisi ya rais.” Mbunge mwingine mweusi kutoka chama cha Democrat, Cedric Richmond, alisema matamshi ya Trump ni dhihirisho tosha kwamba sera yake ya kuliimarisha taifa la Marekani ni sawa na kulifanya taifa hilo kuwa la watu weupe pekee. Aidha, matamshi hayo yamedaiwa kumchefua Mbunge wa Jimbo la Utah kupitia chama cha Republican, Mia Love, amesema kauli ya Rais Trump si yakiungwana wala ubinadamu, pia si kisomi kwani inachafua taswira ya nchi hiyo. Love alimtaka Rais Trump kuomba radhi wananchi wa Marekani haraka iwezekanavyo pamoja na nchi zilizotukanwa. Mia Love ni mbunge wa pekee mwenye asili ya Haiti nchini Marekani. Muungano unaopigania haki za watu weusi, NAACP umemshutumu rais Trump kwa kuzidi kuegemea katika ubaguzi wa rangi. Lakini Ikulu ya Whitehouse imepuuza shutuma hizo zinazomkabili rais. Ofisa mmoja wa Trump, alinukuliwa na Kituo cha habari cha CNN akisema: “Ijapokuwa hili litawakasirisha watu wa Washington, wafanyakazi wanadhani kwamba matamshi hayo yanatokana na mizizi yake, sawa na matamshi yake dhidi ya wachezaji wa NFL waliopiga goti wakati wa kuimbwa kwa wimbo wa taifa.” Msemaji wa ubalozi wa El Salvador mjini Washington, amekataa kuzungumzia kuhusu matamshi hayo. Mhadhiri wa siasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, alitoa maoni yake kutokana na kauli hiyo kuwa pamoja na kwamba Trump kama kiongozi wa nchi hiyo ana haki ya kusema anachotaka, lakini anapaswa kuwa na mtazamo chanya. “Dunia hivi sasa ni kijiji, utandawazi umetufanya tuwe sawa, tuingiliane. Inawezekana ndio kwa hali zetu Waafrika na kuonekana tuko nyuma lakini anatakiwa kuwa na mtazamo chanya kwani Marekani imekuwa kimbilio la watu wengi,” alisema Dk. Bana. Dk. Bana alisema kila nchi ina taratibu zake za kuruhusu wageni na Marekani ni kimbilio la wengi hivyo ni kauli ambayo haipendezi. “Ni kauli ambayo haitupendezi Waafrika ambao bado tunatafuta fursa huko Marekani, lakini ambacho angesisitiza ni utaratibu ufuatwe, sheria zirekebishwe ili zifuatwe lakini si kutubeza kiasi hicho,” alisema Dk. Bana. Alisema anadhani watunga sheria wa nchi hiyo wanapaswa kuliona hilo na kutunga sheria zisizobagua au kuonesha Trump ana chuki ya pekee na watu wenye ngozi nyeusi. Trump akanusha Jana, Rais Trump, alikanusha suala hilo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter. “Maneno niliyoyatumia katika kikao changu na wabunge kuhusu masuala ya uhamiaji (DACA) yalikuwa makali, lakini sikutumia lugha ya aina hiyo dhidi ya nchi yoyote. Kilichochangia maneno makali ni kutokana na mpango wenyewe uliowasilishwa, unairudisha nyuma DACA.” Katika Twiti nyingine, Trump aliandika: “Sikusema chochote cha kuwadhalilisha Wahaiti au Haiti, ni nchi masikini yenye matatizo. Sikusema wafukuzwe. Hiyo habari imetungwa na Democrat. Nina uhusiano mzuri na wananchi wa Haiti. Pengine tutashuhudia mkutano kati yetu huko mbele, bahati mbaya sina imani.” Hata hivyo, Ikulu ya White House haikuwa tayari kuzungumzia maneno hayo yaliyoandikwa na Rais Trump kupitia mtandao wa kijamii. Serikali ya Rais Trump ilitangaza mwaka jana kuwa itafuta vibali vya muda vya kuishi nchini Marekani ambavyo vilitolewa kwa watu 60,000 kutoka Haiti kutokana na tetemeko la ardhi la mwaka 2010 kuharibu jamii ya nchi hiyo. Pia ilisema watu waliopewa vibali hivyo waliruhusiwa kufanya kazi. KUJENGA UKUTA Seneta Dick Durbin wa Jimbo la Illinois kupitia chama cha Democrat, amesema sehemu ya mpango wa uhamiaji unaopigiwa upatu ni kama kamari ambayo inafaidisha zaidi watu kutoka Afrika na baadhi ya mataifa unapaswa kusitishwa ingawa wataruhusiwa kuomba tena vibali vya kuishi. Durbin amesema watu watakaoruhusiwa kuishi Marekani ni wale waliokumbwa na majanga na kukosa makazi hususani kutoka El Salvador, Guatemala na Haiti. Kwa mujibu wa makubaliano hayo kati ya Seneta Durbin na Seneta Lindsay Graham wa chama cha Republican, wamemweleza Trump kuwa unajumuisha kwenye mpango wa maombi ya fedha dola bilioni 1.6 za awamu ya kwanza ya ujenzi wa ukuta mpakani na misaada kwa wanafamilia walioathirika. Serikali ya Trump imeomba kiasi cha dola bilioni 18 ili kujenga ukuta mipakani wenye urefu wa kilomita 119 ambao utajengwa kwa kipindi cha miaka 10. Wabunge wa Democrats wamesema wanakubali mpango wa kulinda mipaka, wa kuwarejesha kwao wahamiaji 800,000 lakini si ujenzi wa ukuta. Hata hivyo, bado hakujapatikana mwafaka. Botswana yamwita balozi wa Marekani kufafanua Wakati huo huo, Serikali ya Botswana kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa taarifa ya kulaani matamshi ya Rais Donald Trump dhidi ya wahamiaji kutoka Bara la Afrika. Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo iliyotumwa kwa vyombo vya habari, Serikali imeamua kumwita balozi wa Marekani nchini humo ili kutoa ufafanuzi juu ya matamshi ya Trump na kueleza nafasi ya Botswana katika kundi lililomaanishwa na rais huyo wa Marekani. “Leo (jana) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imemuita balozi wa Marekani hapa nchini kutoa ufafanuzi dhidi ya matamshi ya Rais Trump kuwa nchi za Afrika na nyingine ni kama uchafu, katika kikao cha Kamati ya Wabunge wanaoshughulikia masuala ya uhamiaji. “Serikali ya Botswana pia imetaka ufafanuzi kutoka Serikali ya Marekani kupitia Balozi huyo na kuthibitisha kama nchi yetu ni miongoni mwa uchafu unaotajwa. “Botswana inaziomba nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Afrika na nchi zinazoendelea kote duniani kulaani matamshi ya Rais Trump.” | 2 |
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019 kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza. “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake. | 5 |
Ushindi huo umefuta ubabe wa Lipuli iliyowasumbua katika mchezo wa raundi ya kwanza uliochezwa Dar es Salaam, ambapo walitoka sare ya bao 1-1 lakini pia, iliondoa ile dhana ya kutokufungwa kwenye Uwanja wa Samora.Mabao ya Yanga yalifungwa na Papy Kabamba Tshishimbi na Pius Buswita. Ushindi huo wa Yanga unafikisha jumla ya pointi 31, hivyo, itaendelea kubaki nafasi ya tatu iwapo kama Azam itakuwa imeshinda mchezo wake dhidi ya Ndanda uliotarajiwa kuchezwa jana jioni.Kabamba alifunga bao la uongozi dakika ya 19 akimalizia mpira wa Emmanuel Martin aliyekuwa akijaribu kufunga, lakini ulikokolewa na kipa wa Lipuli, Aghaton Anthony na kumkuta mfungaji aliuejaza wavuni.Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, Yanga iliyocheza kwa kasi kubwa huku ikijiamini ilikuwa ikiongoza bao 1-0. Bao hilo la ushindi lilipatikana baada ya kuingia kipa chipukizi Ramadhan Kabwili dakika chache kufuatia kutolewa kwa kipa namba moja, Youthe Rostand aliyeumia.Kipindi cha pili licha ya Lipuli kuchangamka walishindwa kuzitumia nafasi kadhaa walizopata lakini Yanga ilitengeneza nafasi ya pili na kuitumia ipasavyo baada ya kufunga bao la pili dakika ya 55 lililofungwa na Buswita aliyepata pasi ya Obrey Chirwa.Hadi dakika 90 zinamalizika Yanga ilitoka kifua mbele kwa ushindi wa mabao 2-0. Hata hivyo, kipindi cha pili walicheza zaidi kwa kujihami huku Lipuli ikishambulia zaidi bila mafanikio.Michezo mingine iliyochezwa jana ni Singida United ilishinda mabao 3-2 dhidi ya Mwadui, Tanzania Prisons ilishinda 2-0 dhidi ya Njombe Mji na Mbeya City ikishinda ugenini 2-1 dhidi ya Majimaji. Wakati huohuo, Simba leo inashuka dimbani kucheza na Ruvu Shooting jijini Dar es Salaam. | 4 |
Habari zilizopatikana jana kutoka vyanzo mbalimbali ndani ya Yanga vilieleza kuwa, tayari Tiboroha ameandika barua kuelezea uamuzi wake huo.“Ni kweli Katibu ameandika barua ya kuacha kazi, amesema ametingwa na majukumu ya kikazi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hivyo kuomba asitishe ajira yake Yanga. “Mkimpata mwenyewe itakuwa vizuri zaidi, lakini nakuthibitishia amejiondoa Yanga, kwa sasa si Katibu Mkuu tena,” kilisema chanzo chetu, ambacho hata hivyo kilikataa kisitajwe jina lake.Dk Tiboroha alipotafutwa na gazeti hili jana, simu yake ilikuwa ikiita bila majibu, hali ambayo pia ilikuwa kwa Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro ambaye simu yake pia haikuwa na majibu.Hata hivyo, Tiboroha jana alikaririwa na mtandao mmoja akithibitisha kuhusu kuachia ngazi kwake akisema amechukua uamuzi huo ilia pate muda zaidi wa kufanya shughuli zake za Uhadhiri UDSM, kitengo cha Elimu ya Viungo.Tiboroha aliingia Yanga SC Desemba mwaka 2014 akichukua nafasi ya Benno Njovu, ambapo kabla ya hapo alikuwepo Lawrance Mwalusako. | 4 |
Alisema hayo juzi wakati wakati akifungua Maonesho ya 13 ya Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (Sido) Kanda ya Kaskazini, yanayofanyika katika viwanja wa Mashujaa Mjini hapa.Mwijage alisema Serikali ya Awamu ya Tano, imedhamiria kujenga viwanda vingi zaidi hasa mahali ambapo pana malighafi za kutosha.“Serikali ya Magufuli ni ya viwanda, dhima ya miaka mitano ni kujenga uchumi wa viwanda utakaochochea ukuaji wa uchumi na ustawi wa maisha ya wananchi,” alisema.Alisema kwa sasa serikali itatengeneza ajira kwa sababu taifa ni changa huku asilimia 65 ya watu wake ni vijana, ambao wengi wao wana umri usiozidi miaka 35 wanahitaji ajira.“Viwanda vitachochea soko la mazao ya wakulima kwani kwa kupitia viwanda kila atakayejishughulisha atatajirika kwa maana atapata fedha na kipato,” alisema.Alisema lengo lingine la kuingia uchumi wa viwanda ni kutengeneza bidhaa kwa ajili ya mahitaji ya watu na bidhaa hizo zitauzwa ndani na nje ya nchi. Mwijage alisema wakati huu ni muhimu kuangalia nafasi ya Sido, kwani viwanda vingi ni vile vidogo na vya kati.Aliwataka maofisa biashara kuwa makocha katika kuelekeza, kwani lengo ni kuhakikisha Sido inakuwa na nguvu.Alisema sasa wanakwenda kuifufua Sido yenye nguvu, kama iliyokuwa wakati wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambapo ilikuwa na nguvu, tofauti na sasa. Mkurugenzi Mkuu wa Sido, Omar Bakari alisema shirika hilo, linaendelea kubuni mbinu mbalimbali kulingana na mahitaji. | 5 |
Na Ahmed Makongo-BUNDA KUANZIA mwaka 2008 hadi mwaka 2018 jumla ya majangili 4,337 yamekamatwa na askari wa wanyama pori wa kampuni ya Grumeti Reserves, katika mapori ya akiba ya Grumeti na Ikorongo, pamoja na pori la wananchi la Ikona, yaliyoko pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara. Hayo yameelezwa mwishoni mwa wiki na Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Grumeti Reserves, Ami Hamidu Seki, wakati akiwasilisha mada katika Mkutano Mkuu wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara, ambapo alisema kuwa katika kipindi hicho kampuni hiyo ilipata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kufanya jumla ya doria 54, 335 ambapo waliyakamata majangili hao. Alisema kuwa majangili hayo tayari yalikuwa yameshaua wanyama mbalimbali wapatao 2,929, kwa kutumia silahajadi zikiwemo nyaya zipatazo 23,314. “Kampuni yetu imeshapata mafanikio mengi ya uhifadhi wa wanayama pori, kwani kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2003 hadi mwaka 2018, tulifanikiwa kukamata majangili 4,337 ambayo tayari yalikuwa yameshaua wanyama mbalimbali,” alisema. Aidha, alisema kuwa katika kipindi hicho pia walikamata mifugo ya wananchi iliyoingizwa katika mapori hayo ipatayo 275,657, ambapo wamiliki wa mifugo hiyo serikali iliwapiga faini ya jumla ya Sh milioni 255.98 Aliongeza kuwa pia mafanikio mengine ni pamoja na kuongezeka idadi ya wanyama katika mapori hayo kutoka wanyama 15,233 mwaka 2003 na kufikia wanyama 36,321 mwaka jana. Alifafanua kuwa mwaka 2003 wanyama aina ya nyumbu walikuwa 605 na mwaka jana wamefikia 7,709, pofu walikuwa 254 na wamefikia 1,116, tembo walikuwa 355 na kufikia 1,116, twiga 331 na wamefikia 759, kongoni 189 wamefikia 289, swala pala 7,147 wamefikia 9,826, nyamera 5,705 wamefikia 11,995, ngiri 435 wamefikia 2,494. Akizungumzia hali ya ujangili, alisema kuwa bado ni changamoto kubwa kwani pamoja na kufanya doria za mara kwa marana kuyakamata lakini bado ujangili unafanyika. Kwa uapande wake Ofisa Utalii wa Hiofadhi ya Taifa Serengeti, Fred Shirima, alitoa wito kwa waandishi wa habari kufanya utalii katika hifadhi hiyo na kupiga picha kwa ajili ya kutengeneza makala jambo ambalo litasaidia kuitangaza hifadhi hiyo. Wakati huo huo, mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima, aliyekuwa mgeni rasimi katika mkutano huo, aliutaka uongozi wa kampuni ya Grumeti Reserves, pamoja na hifadhi ya taifa ya Serengeti, kuwatumia waandishi wa habari walioko mkoani humo, kwa ajili ya kutangaza mambo ya kimaendeleo wanayoyafanya katika jamii inayowazunguka na nchi kwa ujumla. | 3 |
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa BMT, Mohammed Kiganja alisema kamati hiyo imetokana na mapendekezo yaliyotolewa na wadau wa ngumi katika kikao cha pamoja kilichofanyika Aprili 6, mwaka huu.Aliitaja kamati hiyo ya muda kuwa inaundwa na Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), Yassin Abdallah `Ustaadh’, Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Chaurembo Palasa, Rais wa Shirikisho la Ngumi la Kinyogoli (KBF), Habib Kinyogoli na Rais wa Chama cha Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) Emmanuel Mlundwa.Wengine wanaotoka TPBC Limited ni Nemes Kavishe na Onesmo Ngowi. Kiganja alisema kamati hiyo kwa sasa itaongozwa na Ustaadh na Palasa ambapo baadaye wataamua atakayekuwa mwenyekiti.“Jukumu la kamati ni kutengeneza katiba ya chombo itakayoweka mazingira ya kila taasisi kujiona ni sehemu ya chombo hicho kukiheshimu, kukitii na kukipa ushirikiano,” alisema na kuongeza kuwa anaipa kamati hiyo siku 90 kuandaa katiba hiyo haraka.Pia, alisema itafanya kazi kwa ukaribu na serikali, itaratibu taratibu za mashindano ya ndani na nje na kutengeneza kanuni mbalimbali za chombo na kupendekeza hatua mbalimbali za kuchukuliwa kwa watakaokwenda kinyume dhidi ya taratibu hizo.“Ni mategemeo ya serikali kuanzia sasa kuona misafara yote ya kwenda nje kwa ajili ya ngumi inawekwa wazi kwa kamati na serikali na watakachovuna kitakuwa wazi,” alisema.Alisema anategemea hakutakuwa na malumbano yasiyo ya msingi na yenye kuvuruga mchezo huo, na kwamba litasaidia kuongeza ajira kwa vijana wanaopenda kutumia miili yao kupata kipato.Kiganja alisema iwapo kamati hiyo itashindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kama walivyokubaliana `watatumbuliwa’, kwani dhamira yao ni kuona kuwa ngumi za kulipwa zinakuwa na chombo kimoja kitakachofuata kanuni na sheria zitakazowekwa.Kwa upande wa Ustaadh na Palasa kwa pamoja walishukuru uteuzi huo na kuahidi kutomuangusha Katibu huyo.Ustaadh alisema chombo hicho kitafanya kazi kwa maadili na kuahidi kitawashughulikia mapromota matapeli na kuwafungia. Naye Palasa alisema sio tu mapromota watakaoshughulikiwa, bali hata viongozi wa vyama ambao watashindwa kuzingatia kanuni zitakazowekwa na wadau. | 4 |
MFANYABIASHARA Mustapha Kambangwa (34), mkazi wa Kongowe Mbagala, amefi kishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashitaka manne likiwemo la kuisababishia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) hasara ya Sh bilioni 188.9 kwa kupitia mashine ya kilekroniki ya EFD.Kambangwa alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka katika kesi ya uhujumu uchumi namba 19/2018 mbele ya Hakimu Mkazi, Janeth Mtenga Akisoma mashitaka hayo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Christopher Msigwa alidai kuwa mshitakiwa anakabiliwa na mashitaka manne aliyoyatenda katika siku tofauti kati ya Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, mwaka huu.Alidai katika mshitaka ya kwanza, Kambangwa alijifanya kama mtu aliyesajiliwa kuwa mlipa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) Alidai katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, mwaka huu maeneo ya jiji la Dar es Salaam mshtakiwa alijifanya kuwa amesajiliwa kukusanya kodi ya VAT Sh 188,928,752,166 kwa kujifanya anakusanya fedha hizo kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Katika mashitaka ya pili, Msigwa alidai Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, mwaka huu, Kambangwa kwa udanganyifu alitumia mashine ya kieletroniki ya EFD yenye namba 03TZ842011315 iliyosajiliwa kwa jina la Kampuni ya Abraham’s Group LTD kukwepa kodi ya VAT yenye thamani ya fedha hiyo Katika mashitaka ya utakatishaji fedha, tarehe na kipindi hicho, maeneo ya jiji la Dar es Salaam alijipatia au kujimilikisha fedha hizo alizozipata kutokana na makato ya kodi ya VAT ambazo zilipaswa kutolewa kwa Kamishna wa TRA na mshitakiwa huyo alipaswa kujua kuwa fedha hizo bi zao la kosa la ukwepaji kodi Msigwa alidai katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi,2016 na Novemba 2, mwaka huu maeneo ya Dar es Salaam kwa vitendo vya makusudi vya kukwepa kodi alitumia mashine ya kieletroniki ya EFD na huku akijua kwamba hajasajiliwa kama mlipakodi ya VAT aliisababishia TRA hasara ya 188,928,752,166 Alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.Hakimu Mtega alisema mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo hadi itakapopata kibali cha kuendelea na shauri hilo, hata hivyo, Wakili wa Utetezi, Shamo Shadrack aliomba mahakama kupanga tarehe ya karibu ili kupinga mashitaka hayo dhidi ya mshitakiwa . Upande wa mashitaka ulikubaliana na hoja hiyo na kudai kuwa hauna pingamizi kwa sababu hawajui ni mapingamizi gani yatakayowasilishwa . Hakimu Mtega aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 17, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kuamuru mshtakiwa kwenda rumande kwa sababu mashitaka hayo hayana dhamana | 3 |
MANCHESTER, ENGLAND BAADA ya klabu ya Tottenham kukubali kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya vinara wa Ligi Kuu England, Man City, kocha wa timu hiyo, Mauricio Pochettino, ameweka wazi kuwa hakuna wa kuuzima moto wa wapinzani hao. Hata hivyo, kocha huyo amewatupia lawama wachezaji wake kwa kuruhusu bao la mapema katika dakika ya 14 lililowekwa wavuni na kiungo wao, Ilkay Gundogan, mabao mengine yaliwekwa wavuni na Kevin de Bruyne na Raheem Sterling, aliyefunga mabao mawili. Ushindi huo wa Manchester City unawafanya Tottenham kuwa nyuma dhidi ya vinara hao kwa pointi 21, hivyo kocha huyo anaamini ni kazi kubwa kukipunguza kasi kikosi cha Pep Guardiola. “Naweza kusema Manchester City wameamua kuonesha kwanini wao ni timu bora kwenye michuano hii ya Ligi Kuu, kwa upande wetu ni wazi tulicheza chini ya kiwango, hali hiyo ilichangia kuwapa wapinzani nafasi ya kutufunga bao la mapema. “Hatuna la kusema, lakini ukweli ni kwamba Manchester City walistahili kushinda mchezo huo kutokana na ubora wao wa kikosi pamoja na kocha, hakuna timu ambayo inaweza kuzuia kasi yao, lakini chochote kinaweza kutokea kutokana na kuwa soka ni mchezo wa makosa. “Kwa sasa tunatakiwa kutulia na kuangalia mchezo unaofuata ili kuweza kushinda na kujiweka kwenye nafasi nzuri, ushindani ni mkubwa kwenye michuano hii lakini bado muda upo na tunaamini tutafanya vizuri,” alisema kocha huyo. Baada ya ushindi huo baadhi ya wachezaji wa timu ya Man City, walionekana kwenye chumba cha kubadilishia nguo na huku wakiwaimba Manchester United badala ya Tottenham, wachezaji hao walirekodi video huku wakiimba ‘Paki basi, paki basi’, wimbo huo moja kwa moja walikuwa wanawaimbia wapinzani hao ambao waliwapa kichapo cha mabao 2-1 wiki moja iliyopita. Kwa sasa Manchester City wanaongoza kwenye msimamo wa ligi wakiwa na jumla ya pointi 52 baada ya kucheza michezo 18, huku nafasi ya pili ikishikwa na wapinzani wao Manchester United wakiwa na pointi 38 kabla ya mchezo wa jana. | 4 |
SAN ANTONIO, Marekani MCHEZAJI wa timu ya mpira wa kikapu ya San Antonio Spurs, Pau Gasol, ameelezwa kuwa atacheza kwa muda nafasi ya katikati ambayo itamfanya kuwa mbali na mshambuliaji mwenzake, LaMarcus Aldridge. Nyota huyo kwa sasa anatimiza miaka 15 ya kucheza mchezO huo katika Ligi ya NBA nchini Marekani. Kwa mujibu wa kocha wa timu hiyo, Gregg Popovich, wana mpango wa kutumia aina ya uchezaji wa timu ya Golden State Warriors ambao waliitumia katika michezo ya Western Conference hasa baada ya kumsajili mshindi wa zamani wa tuzo ya MVP Kevin Durant. Hata hivyo, wakati klabu hiyo ilipomsajili Sant Boi kwa usajili wa miaka miwili akitokea klabu ya Texan Franchise msimu uliopita, alitambua angeziba pengo la mkongwe, Tim Duncan. Lakini Mhispania, Gasol alitakiwa kubadili nafasi yake kutokana na hasingeweza kucheza nafasi moja na Boi. Kutokana na ombi hilo kutoka kwa Popovich, Gasol analiona kama mtihani kwake hata hivyo atajaribu kupambana ili kulinda kibarua chake. Gasol amefanikiwa kubeba ubingwa mara mbili wa NBA akiwa na timu ya Los Angeles Lakers, huku akipitia changamoto nyingi ambazo huenda zimebeba katika mabadiliko hayo. Nyota huyo aliwahi kucheza mara sita katika michuano ya nyota wa NBA na kuchaguliwa mara nne katika tuzo ya nyota bora wa NBA. | 4 |
Na Abducado Emmanuel, Dar es Salaam KOCHA wa timu ya Yanga Mbrazil, Marcio Maximo, ni kama amesikia ubora wa washambuliaji wa Simba SC, Paul Kiongera na Amisi Tambwe, hivi sasa ameanza kuwapa programu maalumu mabeki wake wa kati, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani, kuhakikisha wanakabiliana na mashambulizi yoyote ya timu pinzani. Mshambuliaji mpya wa Simba, Kiongera ambaye ni Mkenya, anasifika kwa uwezo wake mkubwa wa kumiliki mpira, kufunga na kugawa mapande ya mabao ‘assist’, ambapo kwenye mechi yake ya kwanza tu dhidi ya Zesco United ya Zambia waliyofungwa mabao 3-0, alifanikiwa kushirikiana vema na Mrundi Tambwe. Hivyo inaifanya safu hiyo ya ushambuliaji ya Simba kuwa kali, ikizingatiwa Tambwe alitisha sana msimu uliopita baada ya kuibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa mabao yake 19 aliyofunga. Kwenye mazoezi hayo maalumu ya mabeki ya jana, yaliyokuwa yakisimamiwa na kocha msaidizi wa Yanga, Mbrazil Leonardo Neiva, mabeki wa kati walihenyeshwa vilivyo kwa kupigiwa mipira ya juu na ya chini, waliyotakiwa kuokoa vyema na kutoka kwenye eneo lao la 18. Cannavaro na Yondani wao ndio walikuwa wakisimama pamoja na kuokoa mipira waliyokuwa wakipigiwa pembeni na ya juu, huku kundi jingine lilikuwa na mabeki wengine wa kati, Rajab Zahir na Pato Ngonyani, ambao nao walikuwa wakitakiwa waokoe kama wenzao, mabeki wa pembeni walikuwa ni Oscar Joshua na Juma Abdul. Kwa mujibu wa programu hiyo, inamaanisha Maximo anawaandaa mabeki wake kukabiliana na aina yoyote ya mashambulizi yatakayofanywa na timu pinzani, ili kuzuia timu yake kufungwa mabao ya kizembe. | 4 |
MUNICH, UJERUMANI KOCHA wa Bayern Munich, Carlo Ancelotti, amedai kuwa ameachiwa kazi nyepesi na aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Pep Guardiola ambaye amejiunga na klabu ya Manchester City. Ancelotti amesema kuwa anaamini atafanikiwa katika klabu hiyo ya Bayern Munich kutokana na Guardiola kuweka njia ya mafanikio ya klabu hiyo. Guardiola akiwa katika klabu hiyo ya Bayern, alifanikiwa kutwaa mataji saba katika misimu mitatu ambayo aliitumikia ikiwa pamoja na kutwaa taji la Bundesliga. Ancelotti amedai kuwa anavutiwa na uwezo wa wachezaji hao ambao umeachwa na kocha Guardiola. “Ni kazi nyepesi sana kwa sasa katika klabu hii kwa kuwa nimewakuta wachezaji wakiwa katika ubora wa hali ya juu. “Ninaamini ubora wa timu hii umeachwa na Guardiola, nimeikuta timu hii ikiwa katika ubora wa hali ya juu, hivyo sina kazi kubwa ya kuifundisha timu hii. “Misingi ambayo imeachwa na Guardiola ninaamini siwezi kuiacha au kuibadilisha kwa sasa kwa kuwa ni mizuri na itanipa mafanikio japokuwa nina mipango yangu ambayo ninaweza kuiweka hapa,” alisema Ancelotti. Bayern kwa sasa inashika nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 16 huku nafasi ya pili ikishikwa na Hertha Berlin ambayo na pointi 13 baada ya timu hizo kucheza michezo sita. “Ninajua kwamba timu yangu inafanya vizuri, nimekuwa nikiiangalia timu hii kwa misimu mitatu iliopita, hivyo kikubwa ni kuendelea na kasi hii kwa ajili ya kuipa mataji,” aliongeza. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 57, aliwahi kuzifundisha klabu kubwa duniani kama vile AC Milan, Paris Saint-Germain, Real Madrid pamoja na klabu ya Chelsea.
| 4 |
MWANAIDI MZIRAY (TSJ) NA TUNU NASSOR-DAR ES SALAAM WATUMISHI saba kati ya 134 wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ambao waliondolewa kazini baada ya kubainika na vyeti vya kughushi, wamerudishwa kazini. Hatua hiyo imefikiwa siku chache baada ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurean Ndumbalo kusema watumishi 450 wameshinda rufaa zao. Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Uhusiano wa MNH, Neema Mwangomo alisema watumishi hao tayari wameandikiwa barua za kurudi kazini. Alisema watumishi sita vyeti vyao vilikuwa na utata baada ya majina yao kuonekana katika vituo vya kazi viwili tofauti. “Watumishi hao walihamia hapa na katika uhakiki wa vyeti majina yao yalionekana katika vituo viwili. “Hivyo walitakiwa kupeleka vyeti halisi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhakikiwa ambako wamejiridhisha na kuwarejesha kazini,” alisema Neema. Msemaji huyo wa MNH alisema watumishi watano walikata rufaa na mmoja kati yao alishinda hivyo naye amerudishwa kazini. Hospitali ya Muhimbili ilikumbwa na sekeseke hilo baada ya tangazo lililosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji, Profesa Lawrence Museru kutaja majina na idara za watumishi ambao walibainika kuwa na vyeti vya kughushi. Tangazo hilo lilisitiza kuwa watumishi walioorodheshwa katika orodha hiyo walitakiwa kujiondoa wenyewe kazini kabla ya Mei 15, mwaka huu. Profesa Maseru alisema iwapo watumishi hao hawakuridhishwa na uamuzi huo wakate rufaa kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kabla ya tarehe hiyo na barua hiyo ni lazima ipitie kwake. Idara zilizoongoza kuwa na watumishi waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi ni Kurugenzi ya Uuguzi (70), ikifuatiwa na Kurugenzi ya Tiba watumishi 20. Nyingine ni Kurugenzi ya Tiba Shirikishi (14), Tehama (11), Upasuaji (4) na Raslimali (2) | 3 |
Na JONAS MUSHI, DAR ES SALAAM WAKAZI wa Mtaa wa Kunguru, Kata ya Goba, Manispaa ya Ubungo, Dar es Salaam wameomba mamlaka kuwabadilishia jina la mtaa wao kwani lililopo haliwafai. Wakizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wa wananchi na Kampuni ya Upangaji na Upimaji Makazi (HUSEA), uliofanyika Shule ya Upili ya Mtakatifu Joseph iliyopo Goba, wakazi hao walisema jina la Kunguru na tabia ya ndege huyo za wizi na uchafu, linaupa taswira mbaya mtaa wao. Kilio cha wananchi hao pia kilisikilizwa na Meya wa Ubungo, Boniface Jacob aliyetakiwa awasaidie kubadilisha jina hilo. Hata hivyo wananchi hao hawakutaja jina jipya ambalo wanalitaka. Akitolea ufafanuzi suala hilo, Meya Jacob alisema hakuna ugumu kwenye kubadili jina ikiwa wengi wataridhia, huku akiwapa utaratibu wa kufuata waweze kutimiza matakwa yao. Alisema wanachotakiwa kukifanya ni kukusanya sahihi zisizopungua nusu ya wakazi wa mtaa mzima na waandike barua kwa halmashauri kuomba kubadilisha jina na kutaja jipya wanalolipendekeza. | 3 |
WAPINZANI wa Yanga kwenye mechi ya mtoano ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika wanatarajiwa kujulikana leo itakapochezeshwa droo mjini Cairo, Misri.Mbali na droo hiyo, pia itachezeshwa droo ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Yanga inashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kutupwa nje ya Ligi ya Mabingwa na Zesco United ya Zambia.Leo, Yanga itafahamu timu itakayokutana nayo katika mchezo wa mtoano kuwania kufuzu hatua ya makundi. Kwa mujibu wa ratiba ya michuano hiyo kutoka kwa Shirikisho la Soka Afrika, CAF, mechi hiyo itachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam kabla ya kurudiana ugenini Novemba 3. Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera alisema yupo tayari kukabiliana na timu yoyote watakayopangwa nayo.Baadhi ya timu ambazo Yanga inaweza kupangwa dhidi yao ni Paradou AC (Algeria), ESAE (Benin), DC Motema Pembe (DRC) na FC San Pedro (Ivory Coast). Pia zipo Pyramids (Misri), Bandari (Kenya), Bidvest Wits (Afrika Kusini), TS Galaxy (Afrika Kusini), Proline (Uganda) na Triangle United (Zimbabwe).Yanga inabidi kujipanga ili kufanya vizuri kwenye mechi hiyo na kufuzu makundi kwani tangu msimu huu umeanza inaonekana kuwa na kiwango cha chini hali inayotishia hata ustawi wake kwenye mechi za Ligi Kuu. | 4 |
MIAMI, MAREKANI KLABU ya Manchester City imejaa hofu juu ya mshambuliaji wake mpya Riyad Mahrez, kuwa anaweza kuukosa mchezo wa Ngao ya Jamii ambao utapigwa Jumapili ijayo dhidi ya wapinzani wao Chelsea. Mchezo huo ni dalili ya kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu nchini England, lakini Mahrez anaweza kuukosa kutokana na kupata majeruhi jana alfajili kwenye mchezo wao dhidi ya Bayern Munich. Mchezaji huyo ambaye amejiunga na Manchester City katika kipindi hiki cha majira ya joto akitokea Leicester City kwa uhamisho wa kitita cha pauni milioni 60, aliisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 3-2, lakini alipata tatizo la enka. “Sijui atakuwa nje kwa muda gani, najua amepata tatizo la enka, lakini tutaona labda hakupata tatizo kubwa sana, kitu ambacho kinanipa wakati mgumu ni kuona mchezaji anaumia, huku wachezaji wengine wakiwa bado wapo kwenye mapumziko baada ya michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi. “Siwezi kuwalaumu wachezaji ambao bado hawajawasili, lakini ninafurahia kile walichokifanya kwenye michuano hiyo ya Kombe la Dunia. Mahrez anaweza kuukosa mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Chelsea, lakini ninaamini tuna kikosi kipana kuweza kuziba nafasi hiyo,” alisema Guardiola. Hata hivyo kocha huyo alieleza sababu ya kumuacha benchi mshambuliaji wake wa pembeni Leroy Sane baada ya kucheza katika mchezo wa kwanza dhidi ya Liverpool. “Sane bado hayupo sawa kiakili, hivyo anatakiwa kufanya mazoezi taratibu ili kuweza kurudi katika ubora wake, lakini wala hana majeruhi yoyote kama watu wanavyodhani,” aliongeza | 4 |
ALIYEKUWA Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa hakuwahi kujaza fomu ya kudai fedha alizokuwa akiikopesha TFF na kwamba alikuwa akilipwa kulingana na utaratibu waliojiwekea kwenye shirikisho hilo. Alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde wakati akiulizwa maswali na Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai.Malinzi alidai hajawahi kutoa maelekezo ya upokeaji wa fedha hizo na kueleza kuwa katika mashitaka ya 16 hadi 25 yanaonyesha alilipwa fedha na TFF. Alidai fedha hizo zililipwa kwa utaratibu na kueleza kuwa hundi na vocha zilizotolewa mahakamani kama ushahidi ni baadhi, kwani zipo nyingine ambazo hazikuletwa mahakamani kama ushahidi. “Niliwahi kufadhili mbio za wabunge kwa miaka saba, nilipromoti ngumi na nilifadhili mchezo wa golf kwa kutumia fedha zilizotoka Cargo Star, lakini sikuwahi kueleza chanzo cha mapato yake,” alidai Malinzi. Malinzi bado anaendelea kuhojiwa kutokana na ushahidi wake wa utetezi. Hakimu Kasonde aliahirisha kesi hiyo hadi leo kwa ajili ya kuendelea na hatua ya usikilizaji upande wa utetezi. | 4 |
Na Mwandishi Wetu-ZANZIBAR HATUA ya Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto, Maudline Cyrus Castico, kutangaza mabadiliko ya kima cha chini cha mishahara kwa sekta binafsi bila kushirikisha wawekezaji wa sekta ya utalii, sasa hatima yake ipo mikononi mwa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein. Mbali na hilo, inaelezwa kuwa Waziri Castico amechukua uamuzi huo bila kushirikisha hata baadhi ya viongozi wenzake ndani ya Serikali pamoja na Baraza la Wawakilishi (BLW) kama sheria inavyotaka. Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi, Mohamed Said Dimwa, alisema licha ya hali hiyo lakini bado kamati yake haijahusika na mabadiliko hayo ambayo huenda yakaleta hatari kwa Wazanzibari wengi kupoteza kazi kupitia sekta ya utalii. Alisema uamuzi uliochukuliwa wa kuongeza mishahara kwa sekta binafsi ni wa Waziri Castico binafsi na si wa Serikali na huenda una lengo binafsi lililojificha ndani yake. “Nasisitiza tena suala hili halijapita kwenye kamati yetu ya bajeti na kwa sababu suala hili ni kama lisingepita kwetu lingekwenda katika Kamati ya Sheria ndogondogo napo huko nami ni mjumbe lakini pia sijaliona tukijadili. “Kwa hali hiyo kinachofanyika sasa ni kuomba Spika wa Baraza la Wawakilishi kwa kumwandikia barua ili kuweza kujadili suala hili kwa haraka kwa kibali chake na kama tukiacha hali hii kuna hatari kubwa kwa wafanyakazi wengi hasa Wazanzibari kupoteza nafasi za ajira kupitia sekta hii. “…siku zote tunasisitiza kukuza hali bora ya maisha kwa Wazanzibari kama Ilani ya Uchaguzi inavyotuelekeza, tusipochukua hatua za haraka kuna hatari ya kuwarudisha nyuma na kuzuka kwa malalamiko toka kwa wananchi,” alisema Dimwa. Mshauri wa Rais Kutokana na sintofahamu hiyo, MTANZANIA lilizungumza na Mshauri wa Rais wa Masuala ya Uchumi, Balozi Mohamed Ramia, ambaye naye alikiri kusikia suala hilo huku akiahidi kulifuatilia suala hilo kwa undani. “Hili suala ….. nitalifuatilia ili nione limekaaje,” alisema Balozi Ramia. Hata hivyo, mmoja wa kiongozi wa SMZ ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini, alisema kuwa licha ya suala hilo kutishia hali ya uchumi wa Zanzibar tayari Rais Dk. Shein, amepewa taarifa huko alipo pindi atakaporejea nchini Julai 25, huenda akatoa uamuzi wa Serikali. “Ingawa Rais (Dk. Shein) yupo nchini Uingereza kwa ziara maalumu, ila ninachokuhakikishia kila siku anapata taarifa ya kinachoendelea nchini. Na kuna hatari hata kiongozi anafanya haya mabadiliko huenda hata akapoteza kazi kama hakujipanga vizuri. “Mapato ya Zanzibar kwa asilimia 80 yanatokana na sekta ya utalii, maeneo mengine huchangia kiasi lakini si kama sekta hii, hivyo ukiiyumbisha na watu kupoteza ajira kiuchumi Zanzibar itarudi nyuma kuliko ilipo sasa,” alisema kiongozi huyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini. Katibu wa BLW MTANZANIA lilimtafuta Katibu wa Baraza la Wawakilihi (BLW), Raya Issa Mselem, ambaye alisema kwa sasa anahitaji kufuatilia kwa undani ili kujua suala hilo kama limepita katika kamati ya bajeti ama la. “Kwanza binafsi nilisikia tu tamko la Waziri mwenye dhamana (Maudline Cyrus Castico) kuwa kuna nyongeza ya mabadiliko ya mishahara kwa sekta binafsi sasa kujua kama limepita kwenye kamati hili sifahamu. “Unajua hizi kamati za kisekta hata kama hazijadili suala hili lakini pia huangaliwa sera na sheria kwa kuona je, ana nguvu kisheria. Na kazi ya kamati ni kutoa maoni na ushauri kwa Serikali wafanye nini. “Ila kwa kuwa suala hili sijalifuatilia sana siwezi kusema kama limejadiliwa ama la. Jambo la msingi kuangalia nguvu ya kisheria ambayo imepitishwa na Baraza la Wawakilishi ambalo ndilo lenye uwezo kwa mujibu wa sheria,” alisema Raya. Waziri Abood Alipotafutwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Abood, alisema kwa sasa bado wanaendelea kulifanyia kazi suala hilo kwa ngazi ya Serikali ikiwamo kukutana na wawekezaji wa utalii Zanzibar ili kusikia kilio chao. Ingawa hakutoa ufafanuzi wa kina taarifa zinaeleza kuwa kesho Serikali itakutana na wawekezaji wa utalii ili kujadili suala hili na kutafuta ufumbuzi wa pamoja. Waziri Castico MTANZANIA lilipomtafuta Waziri Castico ili kujua msimamo wake kuhusu hilo, hakuwa tayari kuzungumzia na alipotafutwa kwa njia ya simu iliita bila kupokewa. Hata hivyo, katika msimamo wake alioutoa wiki iliyopita alipokuwa akizungumza na MTANZANIA, alisema kwa sasa Serikali inalifanyia kazi suala hilo na anaamini ufumbuzi utapatikana licha ya wadau kutoa maoni yao. Inaelezwa kuwa suala hilo la mabadiliko ya mishahara kwa sekta binafsi alimshirikisha pia Waziri wa Utalii pamoja na fedha ambao hata wanapotafutwa ili kupata kauli zao hawako tayari kuzungumzia suala hilo. Hali ya uchumi Sekta ya utalii imekuwa ikichangia asilimia 7 ya pato la uchumi Zanzibar, ambapo Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Khalid Salum Mohammed, alinukuliwa akisema pamoja na ukuaji wa uchumi wa Zanzibar kuimarika, lakini bado ukuaji wa uchumi huo hauendani na ongezeko la idadi ya watu katika visiwa hivyo. Alisema kasi yao ya ukuaji wa uchumi ipo karibu asilimia 6.7 na walioitarajia ni asilimia 7.2 kwa mwaka 2017, lakini anahisi ingekuwa zaidi ya hapo kwa vile ongezeko la idadi ya watu ambalo kwa sasa limefikia asilimia 2.8 ikiwa ni karibu na asilimia tatu. “Sasa bado kasi yetu inakuwa lakini ninahisi kwamba ingekuwa zaidi ya kiwango hicho tulichokipangia, tunakuwa kwa asilimia 2.8 karibu tatu lakini ili kuweza kumudu mahitaji ya watu basi tunahitaji uchumi wetu ukuwe kwa asilimia 10 kupitia dira yetu ya maendeleo ya 2020 ambayo bado hatujaifikia,” alisema. Mishahara Serikali ilitangaza kuanzia Julai Mosi mwaka huu kuwepo kwa mabadiliko ya kima cha chini kwa wafanyakazi wenye mikataba ya maandishi kwa taasisi ndogo zitakazoainishwa kwenye kanuni kimeongezeka kutoka Sh 145,000 hadi 180,000. Kwa wafanyakazi wenye mikataba ya maandishi imeongezeka kutoka kiwango cha sasa cha Sh 145,000 hadi 300,000. Huku kwa vibarua wa kutwa wenye ujuzi, kimeongezwa kutoka Sh 10,000 hadi 30,000 kwa siku na kwa vibarua wa kutwa wasio na ujuzi, kimeongezwa kutoka Sh 7,000 na kufikia 25,000. | 3 |
Na RAMADHANI MASENGA BADO unasikia watu wakitaka kushindanisha muziki wa Singeli na Bongo Fleva? Bado unahisi Singeli una msisimko kwa watu wa kariba zote kama ilivyotaka kutokea miezi michache iliyopita? Muziki wa Singeli umedumaa. Wasanii wake wameshindwa kuwaza kiubunifu na matokeo yake bado wanaufanya kuwa muziki wa tabaka lilelile. Tabaka la wahuni na masela wa kitaa. Ili muziki uweze kuwa na mafanikio makubwa ni lazima uwe na taswira njema kwa jamii. Unaiona Bongo Fleva ya leo? Miaka karibu ishirini iliyopita ulikuwa muziki wa watu fulani. Wahuni fulani na masela fulani. Ulikuwa na mafanikio? Hapana. Japo ulishabikiwa na vijana kwa nguvu ila haukuwa na mafanikio. Kina Sugu, Juma Nature na wenzao walikuwa na majina makubwa ila yasiyo na heshima wala mafanikio ya maana. Baada ya miaka kadhaa, wakabadili namna ya kuandika mashairi yao. Sasa watu wakaanza kuvutiwa. Ukatoka kuwa muziki wa masela na vijana wa vijiweni, mpaka kuingia katika majumba ya kishua na vyuoni. Sasa hata wasomi wakaanza kuona Bongo Fleva ni muziki wa maana. Wale wazazi waliokuwa wakidhani muziki huu ni uhuni wakatoa mawazo yao na kusapoti vijana wao kujiingiza katika muziki huo. Sasa haishangazi kuona msanii wa muziki huu akiitwa Ikulu na mkuu wa nchi. Tumeshuhudia wanamuziki wa muziki huu wakiwa wabunge na mabozi wa taasisi na kampuni kadhaa. Kuna sehemu muziki wa Singeli upo. Wanamuziki na wadau wake wakiacha kuwa makini muziki huu utakufa ungali bado mchanga. Mpaka sasa muziki wa Singeli upo kiburudani na mambo mengine ya hovyo. Angalia wanamuziki wakali wa Singeli na nyimbo zao. Yupo Man Fongo. Wimbo wake uliotamba sana ni Hainaga Ushemeji. Ni wimbo mzuri kuusikiliza lakini hauna maadili. Kuna Sholo Mwamba. Naye yuko katika mfumo huohuo. Na sasa Msaga Sumu katoa wimbo mwingine ‘Mwanaume Mashine’. Ukisikiliza huo wimbo toka mwanzo mpaka mwisho ni lazima ugeuke nyuma kuangalia unasikiliza na wangapi. Siyo wimbo wa kusikiliza na wazazi au yeyote unayemuheshimu. Lakini wadau wake wanasema ni mzuri. Hatari ya mambo kama haya ni kudumaza muziki wenyewe. Kama muziki huwezi kudhaniwa kusikilizwa na jamii staarabu, unategemea vipi wazazi kuwaruhusu vijana wao kuushiriki muziki huo? Katika hali kama hiyo, unategemea vipi wadau makini, zikiwemo kampuni kuendelea kuweka hela katika muziki huo? Kama kuna ndoto ya kubadilisha muziki huo na kuwa wa kibiashara zaidi, wadau hawana budi kubadlika. Badala ya kuimba ilimradi tu watu wacheze bila kujali aina ya maneno ama maudhui ya wimbo husika, sasa ni zamu ya watu kuanza kufikiri kwa kina na kutoa nyimbo makini za kufaa watu kusikiliza na kujifunza kitu. Bongo Fleva leo inatamba kimataifa kwa sababu ndani ya nchi huu muziki una heshima yake. Kina Proffesa Jay, Sugu na Ferooz wameimba nyimbo za kuelimisha na kuburudisha jamii. Leo hata waziri akisikia mwanaye anataka kujiingiza katika muziki wa Bongo Fleva hawezi kushtuka. Atashutuka vipi wakati ndani kuna kina Ferooz, Afande Sele, Maalim Nash na Diamond? Ndani kuna waelimishaji na wafanyabiashara wakubwa. Katika Singeli kuna nini? Bado kuna Mwanaume Mashine, Mwaga Maji Tucheze Kama Kambale na Hakunaga Ushemeji. Aibu hii. | 1 |
Alitoa kauli hiyo juzi usiku wakati akizungumza na mabalozi na wageni mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya miaka 70 ya Uhuru wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam na miaka 50 ya kuanzishwa kwa mahusiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na Vietnam, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.“Huu ni wakati muafaka kwa nchi zetu kuangalia ni aina zipi za uwekezaji zinafaa kuchukuliwa kwa manufaa ya nchi zetu na wananchi wake. Nitumie fursa hii kuwakaribisha wawekezaji kutoka makampuni ya Ki-Vietnam waje kuwekeza kwenye usindikaji wa korosho, utengenezaji wa saruji na viwanda vya nguo,” alisema Waziri Pinda.Aliyataja maeneo mengine ambayo wenye kampuni wanaweza kuwekeza kuwa ni nyanja ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) pamoja na ujenzi wa nyumba za kuishi.Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuipongeza kampuni ya mawasiliano ya simu ya Vietnam (VIETTEL) kwa uamuzi wake wa kutenga Dola za Marekani bilioni moja ambazo zitatumika kuendesha shughuli zake nchini.“Huu ni mtaji mkubwa sana, siyo tu hapa Afrika Mashariki na Kati bali hata barani Asia. Uwekezaji huu utazalisha ajira za moja kwa moja 1,700 na ajira nyingine 20,000 ambazo si za moja kwa moja,” aliongeza.Kwa upande wake, Balozi wa Vietnam nchini Tanzania, Vo Thanh Nam alisema tangu ipate uhuru wake hadi, nchi hiyo imekwishaanzisha uhusiano wa kidiplomasia na nchi 185 na wakati huo huo imekwishaweka uhusiano wa kibiashara na uwekezaji na nchi 220. | 5 |
Na Mwandishi Wetu-Zanzibar WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Watanzania washirikiane katika kuulinda na kuutetea Muungano wa Tanzania na Mapinduzi ya Zanzibar na kamwe wasiruhusu watu kuingiza sumu ya kutaka kuwagawa. Aliyasema hayo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi katika mikutano iliyofanyika Wilaya ya Kati na Wilaya ya Kusini alipokuwa katika ziara yake ya kikazi mkoa wa Kusini Unguja. “Watanzania tusikubali mtu yeyote kutugawa kwa sababu sisi undugu wetu ni wa damu, ni vema tukaendelea kuudumisha muungano wetu, tusiruhusu watu kuingiza sumu ya kutaka kutugawa kwani watu hao hawana tija,” alisema Majaliwa. Waziri Mkuu ambaye awali alikagua miradi mbalimbali ikiwamo ujenzi wa maabara ya sayansi katika Shule ya Sekondari Bwejuu, mradi wa kilimo cha kisasa Jozani na kuzindua jengo la mama na mtoto Bambi alisema hayo ni matunda ya muungano, hivyo hawana budi kuendelea kuudumisha. Akikagua maendeleo ya ujenzi wa maabara ya sayansi katika Shule ya Sekondari ya Bwejuu, Waziri Mkuu alitoa muda wa miezi mitatu kwa mkandarasi anayejenga maabara hiyo awe amekamilisha kazi hiyo. Pia alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Ayoub Mohammed Mahmoud, ahakikishe watumishi wanatenga muda wa siku nne kwa wiki kwenda kuwahudumia wananchi katika maeneo yao, hususan ya vijijini. Vilevile, aliagiza maofisa kilimo wahamishiwe vijijini ili waweze kuwasimamia wakulima, ikiwa ni pamoja na kuwashauri namna bora ya kulima kwa kufuata kanuni na matumizi mazuri ya pembejeo. Kadhalika, alisisitiza umuhimu wa kutoa huduma kwa wananchi wote bila ya kujali dini, kabila, rangi wala itikadi za chama kwa kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi wote wananufaika na kuhudumiwa bila ya kubaguliwa kwa namna yoyote. Awali, viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani wakiwamo wa CUF, NRA, UPDP, NCCR-Mageuzi waliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa kuimarisha huduma za kijamii. Viongozi hao walisema wapo tayari kushirikiana na Rais Dk. John Magufuli pamoja na Rais Dk. Ali Mohamed Shein kwa sababu viongozi hao wanafanya kazi nzuri ya kuwahudumia wananchi. “Maendeleo hayana chama, naunga mkono jitihada zinazofanywa na SMT na SMZ na nimefurahia ziara ya Waziri Mkuu hapa kisiwani Unguja na ninamuunga mkono Rais Dk. Magufuli, tumepata maendeleo ambayo hatukuyatarajia,” alisema Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa NRA, Khamis Faki katika mkutano wa hadhara uliofanyika Shehia ya Bambi. | 3 |
Waandishi Wetu- mikoani, Dar na mikoa VIONGOZI mbalimbali wametoa kauli nzito juu ya kushamiri kwa matukio ya ukatili wa kingono ambayo yamezidi kushamiri siku hadi siku Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema matukio ya ukatili wa kingono yanayoendelea kutokea kwa kasi nchini ambayo wanayofanyiwa wanawake na watoto wa kike, ni sawa na uhujumu uchumi. Alisema kuendelea kushamiri kwa matukio hayo, ni kurudisha nyuma jitihada za Serikali za kuhakikisha inapambana na matukio ya ukatili wa kijinsia ikiwemo kufikia usawa wa kijinsia. Samia alisema hayo jana, wakati akizungumza na na mamia ya wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa maazimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yalifanyika mkoani hapa. Alisema matukio hayo, yamekuwa yakiwahathiri watendewa, bali waathirika wengine ni familia, jamii na taifa kwa ujumla, kutokana na idadi kubwa ya watendewa kuwa ndiyo wazalishaji wakubwa. Alisema kumekuwepo na ongezeko la matukio hayo kutoka ambayo uripotiwa kwenye vituo vya polisi, kutoka matukio 31,996 mwaka 2016 hadi matukio 43,487. Alisema ili vitendo hivyo viweze kupungua kama siyo kuisha kabisa, lazima jamii yote kwa ujumla iweze kupambana kupiga vita matukio haya ikiwa pamoja na wahusika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. “Hii hali ni mbaya, taifa letu linaelekea kwenye hali mbaya, kila mmoja wetu achukue nafasi yake kuhakikisha anamlinda mtoto wake na mtoto wa jirani, kila mmoja apambane na vitendo hivyo, serikali peke yake haiwezi lazima kila mmoja apige vita,” alisema Samia. Alisema inaendelea kutekeleza maazimio ya mkutano wa wanawake Beigin China uliofanyika mwaka 1995, ambapo katika upande wa usawa wa kijinsia kwenye elimu na mafunzo serikali inatoa elimu bure shule za msingi na sekondari. Alisema utekelezaji wa sera hiyo ya elimu bure, itaondoa ubaguzi wa kielimu uliokuwepo kati ya mtoto wan a kiume, ambapo alisema serikali itawachukulia hatua kali wale wote ambao wanaowakataza watoto kwenda shule. Alisema Serikali imekuwa ikiwawezesha wanawake kiuchumi, kupitia halmashauri kwa kuwapatia mikopo kupitia makusanyo ya mapato ya ndani asilimia 10, ambapo zaidi ya bilioni 9.7 zimetolewa kwa vikundi 14,870. Katika kupunguza umaskini kwa wanawake, Makamu wa Rais alisema kuwa serikali ilianzisha mpango wa kunusuru kaya Maskini awamu ya tatu (TASAF III) ambapo asilimia kubwa ya walioko kwenye mpango huo ni wanawake. Alisema serikali imeendelea kuwapa nafasibalimbali wanawake katika siasa na nafasi za uongozi, huku akiwasisitiza wanawake nchini kutumia fursa ya uchaguzi mkuu mwaka huu katika kuchukua fomu kugombea udiwani na ubunge. Mratibu wa Umoja wa Mataifa, Zlatan Milisic, aliipongeza Serikali kuwawezesha wanawake kwenye nyanja za uongozi na uamuzi. Alisema Tanzania imetia saini makubaliano ya Jukwaa la Beijing pamoja na sheria nyingine za dunia ambazo zinahamasisha usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake na wasichana. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu alisema kuwa ajenda ya usawa na jinsia na uwezeshaji siyo ya wanawake tu bali ni watu wote wakiwemo wanaume. Ofisa Mtendaji wa Mkuu wa Chama cha wafanyabishara Wanawake Tanzania (TWCC), aliwataka wanawake nchini kutumia maazimisho hayo katika kujitadhimini walipo na kuweka mikakati ya kuboresha mbinu za kufikia malengo ya mafanikio kwa baadaye. Ofisa Habari na mahusiano Shirika la Word Vision Agness John, alisema kuwa wameendelea kuwasadia wanawake kupitia vikundi vya ujasliamali katika ili kuondokana na matukio ya ukandamizwaji katika jamii na familia kwa jumla. MAKONDA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema kuazia leo (jana), atawashughulikia kikamilifu wanaume wenye tabia ya kuwaonea wanawake kwa kuwapiga hadi kuwaharibu mwonekano wa sura, macho,kuwavunja meno au taya na kusababisha baadhi yao kupata ulemavu wa kudumu jambo ambalo ni kinyume na Sheria. Alisema mwanamke yoyote atakayeshushiwa kipigo na mwanaume kuanzia sasa atoe taarifa kupitia simu ya mkononi. Alisema baadhi ya wanaume wamekuwa na tabia ya kuwadharau wanawake kutokana kutokuwa na elimu au kipato jambo ambalo alisema hawezi kulivumilia katika mkoa huo. “Kiongezwe kipengele cha kutaka asilimia asilimia 40 ya mshahara wa mwanaume apatiwe mwanamke asiefanya kazi kwa ajili ya shughuli za familia ili kumsaidia kumjengea uwezo,” alisema Makonda. CUF Jumuiya ya Wanawake ya Chama cha Wananchi (CUF),imeiomba Serikali kuanzisha sera madhubuti zitakazoamuru kila shule kuwe na utaratibu wa kugawa taulo za kike bure ili kuchochea ufaulu kwa wanafunzi wa kike. Katibu wa Jumuiya hiyo, Anna Paul alisema, zipo sababu nyingi zinazochangia kushuka elimu kwa watoto wa kike, ikiwamo mazingira ya kimaumbile wanayokabiliana nayo. Alisema ili kuwajengea umakini wakiwa darasani, ni vema kukawekwa utaratibu maalum utakaompa uhakika mwanafunzi huyo wakuwa safi na salama pindi anapokuwa kwenye hedhi. JOKETI Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe,Joketi Mwegilo aliwataka wanawake kujiamini, kujituma na kujenga familia bora kwa kufata misingi ambayo itawasaidia kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazowakabili pindi wanapokumbana nazo. Alisema wanawake wanatakiwa kuacha kujibweteka na kuchukulia changamoto kama chachu ya maendeleo katika katika nyazifa zao na jamii kiujumla. Alisema wanawake wanapokuwa kwenye uongozi au utendaji hawatakiwi kuogopa changamoto wanatakiwa kuzikabili. “Wanawake wanatakiwi kutokujiweke nyuma wanatakiwa kujishughulisha na kujikita kwenye biashara jiwezeshe na kujiunga kwenye vikundi mbali mbali vitakavyo kusaidia kupata mikopo,”alisema Alisema alipoteuliwa kwenye nafasi ya kuwa mkuu wa wilaya wapo watu wakisema kuwa mdogo awezi kufanya kazi katika ngazi hii. Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kisarawe, Eve Station alisema ni wakati wa mwanamke kuishi kwenye ndoto na kipaji chako sio, unapoolewa tu unakatishwa kipaji chako tuinuke na tulete maendeleo kwenye nchi yetu. JKCI Ofisa Lishe wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Maria Samlongo amewataka wanawake kuzingatia lishe bora katika familia zao ili kuepukana na magonjwa ya moyo. Alisema lishe bora kama sehemu ya kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ikiwemo magonjwa ya moyo. “JKCI tunamchukulia mwanamke kama sehemu muhimu katika magonjwa ya moyo, anatumika kununua chakula,kukipika au kuandaa mpaka kinafika mezani,”alisema. TANGA Huko mkoani Tanga, wametakiwa kuchangimkia fursa ya kauli mbiu ya awamu ya tano kuelekea uchumi wa viwanda kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo na vikubwa ili kuweza kujikwamua kiuchumi wao na jamii zinazowazunguka. Hayo yalisemwa jana na Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga, Specioza Owure. Alisema kina mama wasilaze damu kwa kuhakikisha wanachangamkia fursa, ikiwemo kujiunga kwenye vikundi na kuanzisha viwanda ambavyo vitakuwa chachu kubwa ya kufikia mafanikio na kuweza kuwainua kiuchumi. KATAVI Taarifa kutoka mkoani Katavi, zinasema wanawake wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Mkoa, wametowa msaada kwa mahabusu wa kike walioko gereza Mpanda, ikiwemo mashine ya kisasa ya kunyolea nyele itakayosaidia usalama wao. Akikabidhi misaada hiyo kwa niaba ya wanawake wa chama hicho, Makamu Mwenyekiti wa TUGHE, Mary Buberlwa alisema wameona ni vema kile kidogo walichonacho waweze kuwasaidia wenzao waliko mahabusu ili kuwapa moyo na nguvu wasijifikirie vibaya kuwemo kuwa mahabusu | 3 |
Zawadi hizo zitatolewa katika promosheni ya Kampuni ya Coca Cola kupitia Kiwanda cha Bonite Bottlers. Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Bonite Bottlers, Chris Loiruk alisema jana kuwa kampuni ya Coca Cola ni mdhamini mkuu wa mashindano yajayo ya Kombe la Dunia, ambayo yanakaribia kuanza.“Tumewaandalia promosheni hii wakazi wa Kanda ya Kaskazini ili kuhakikisha wanafurahia ‘Mzuka wa Soka na Coka’ wakiwa majumbani kwao kupitia runinga za kisasa wakati huohuo wakiburudika na vinywaji vya Coca Cola” alisema wakati wa uzinduzi wa promosheni kubwa.Loiruk alieleza kuwa promosheni hiyo mpya, itanufaisha watumiaji wa vinywaji vinavyotengenezwa na kampuni ya Coca-Cola ambavyo ni Coca-Cola, Sprite, Fanta, Sparletta, Schweppes, Stoney Tangawizi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Tanga na Singida.Mbali na kujishindia runinga bapa za kisasa, watumiaji wa vinywaji vya Coca Cola watazawadiwa zawadi za pikipiki, fedha taslimu kuanzia shilingi 5,000 hadi Sh 100,000 pamoja na soda za bure.Meneja wa chapa ya Coca Cola nchini Tanzania, Sialouise Shayo alisema promosheni hiyo imelenga kuwaandaa washabiki wa soka nchini, kujiandaa kufurahia mzuka wa kombe la Dunia na kufurahia mashindano hayo pindi yatakapoanza.“Tukiwa wadhamini wakuu wa mashindano ya Kombe la Dunia yatakayoanza mwezi Juni mwaka huu, tumeona kuna umuhimu wa kuwaletea wateja promosheni itakayowaunganisha na kufurahia mashindano haya makubwa duniani kupitia kunywa soda zetu,” alisema. | 4 |
SIMBA tayari imemaliza kazi moja na inatarajia kuanza nyingine mpya kabisa. Ndiyo, wamemaliza vyema safari ya kupambana na kuingia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika! Simba imeingia hatua hiyo baada ya kucheza mechi nne za kimataifa na sasa inatembea kifua mbele ikitamba kila kona, si wachezaji wala viongozi.Siyo mashabiki wala wanachama lakini pia hata watanzania wenye mapenzi ya kweli na soka la nyumbani wamekuwa na msisimko wa kutosha kwa Simba kufika hatua hii. Si kwamba wekundu hao wamebahatisha kupata mafanikio hayo kidogo ambayo ni makubwa kwa sasa ukilinganisha na mara ya mwisho timu za Tanzania kufika hatua hiyo. Nitakwambia kwa nini? Ila kwa faida yako mara ya mwisho Tanzania kufikia hatua hii ilikuwa 2003 na Simba hii ndiyo ilipindua meza kibabe.Kwanza, ilimnyoosha bingwa mtetezi wa wakati huo, Zamalek ya Misri na kutinga hatua ya makundi na sasa imerudia tena makali yake hayo baada ya kupita miaka 15 bila Tanzania kuonekana katika hatua ya makundi ya michuano hiyo mikubwa kabisa kwa ngazi ya klabu Afrika. Turejee kwa nini Simba haikubahatisha kufanya hivyo. Msingi wa timu hiyo, tangu inaanza kufanya mabadiliko ya uongozi, wimbo wao mkubwa ulikuwa ni kufika hatua kubwa ya kushiriki michuano ya kimataifa.Bilionea Mohamed Dewji ‘Mo’ambaye ni mwekezaji mwenye hisa asilimia 49 kwa klabu hiyo alipambana kwa kila namna pamoja na viongozi wengine wa timu hiyo kuhakikisha wanakuja wachezaji wakali na wanapata wanachokihitaji ili mambo tu yaende sawa. Haikuishia hapo, benchi la ufundi la timu hiyo lilipigwa msasa wa kutosha kama siyo kusafishwa vyema ili tu apatikane mtu sahihi atakayewaongoza kufika nchi ya ahadi ambayo sasa Simba ipo.Ilianza mtihani wake wa kwanza kwa timu ngumu ya eSwatini, Mbabane Swallows ingawa safari hii ilionekana kuyumba na Simba ikatumia mwanya huo bila ya kupoteza muda na kuifumua mabao 4-1 katika mechi ya kwanza ailiyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mabao yalifungwa na John Bocco, Clatous Chama na Meddie Kagere. Katika mechi ya pili iliyopigwa kwenye ardhi ya Mfalme Mswati, Simba iliamua kufanya maajabu hukohuko ugenini kwa kuwabubujua wapinzani wao kwa mabao 4-0.Katika mechi hii, Chama aliweka mabao mawili murua na kisha Emmanuel Okwi na Kagere wakakandamiza moja kila mmoja. Hatua iliyofuata, wakakutana na Nkana FC kutoka Zambia. Hapa haikuwa shughuli nyepesi na hapa ndipo Simba ilipoonesha kwa kiasi gani ilikuwa na kiu ya mafanikio ya kufika katika hatua ya makundi. Ilianza kwa kipigo kule Kitwe, Zambia kwa kuchapwa mabao 2-1.Licha ya Simba kukukuruka na kupambana kutengeneza nafasi nyingi lakini Nkana walisimama imara katika ardhi yao ya nyumbani na mwisho Simba ikaondoka Zambia kichwa chini. Hazikuwa hisia nzuri kwa watanzania hasa mashabiki wa Simba, waliamini hawana chao na shughuli ndiyo imeishia hapo. Historia ya Nkana dhidi ya Simba haikuwa nzuri hata kidogo. Hapo awali Simba haikuwahi kukutana na Nkana na ikatoka salama na mara zote wamekuwa wakizidiwa bao moja tu katika matokeo ya jumla mwisho kutupwa nje ya mashindano.Lakini safari hii, historia haikufanya kazi na hisia mbaya pia hazikuwa na nguvu zaidi ya matumaini na mapambano ya kweli yaliyojaa mioyoni mwa wachezaji wa timu hiyo, ndicho kilichoirejesha Simba kwenye ramani ya soka la Afrika. Mechi ya pili iliyopigwa kwenye uwanja wa Taifa z utata huo. Maelfu ya mashabiki walijitokeza kuipa nguvu timu yao ingawa mapema walianza kukatishwa tamaa na kuamini hawana chao baada ya dakika ya 17 ya mchezo, Walter Bwalya kuipatia Nkana bao la kuongoza na kuifanya mechi kuwa ngumu zaidi. Katika mechi hiyo, Simba ilihitaji ushindi wa bao 1-0 pekee ili isonge mbele kwa kuwa walikuwa wakilindwa na lile bao moja la ugenini walipofungwa 2-1.Lakini kwa bao la Bwalya, Sasa Simba ilihitaji ushindi wa mabao kuanzia matatu huku wakiwa hawajaruhusu jingine ili ikate tiketi ya kuingia makundi. Simba ilijitutumua na kuamini bado wana nafasi. Jonas Mkude aliyelelewa na kukulia katika timu ya vijana ya Simba kwa muda mrefu akiwa hajaifungia bao timu hiyo, siku hiyo ndiyo ilikuwa wakati wake wa kulipa fadhila kwa kupiga shuti nje ya 18 na kumzidi mlinda mlango wa Nkana na mpira kujaa wavuni dakika ya 29. Shangwe zenye matumaini finyu zililipuka na Simba wakacharuka wakitandaza kabumbu huku wakilisakama lango la wapinzani hao na zikiwa zimesalia sekunde chache kwenda mapumziko, Kagere akaiandikia Simba bao la pili.Kazi ikawa imelainika lakini ikahitajika shughuli ya ziada ili kuwa na uhakika juu ya hilo. Baada ya vuta nikuvute, wengi wakiamini mshindi ataamuliwa kwa matuta kama ilivyotokea mwaka 2003 wakati Simba inaingia hatua ya makundi kwa mara ya mwisho, Clatous Chama akaiandikia Simba bao la tatu dakika ya 88. Lilikuwa bao safi, litakalobaki kwenye kumbukumbu ya watanzania wengi kwa miaka mingi kuliko unavyofikiri. Alifunga kwa kisigino chepesi akiwahadaa kipa na beki wa Nkana baada ya kupokea pasi ndani ya 18 kutoka kwa Hassan Dilunga.Huo ukawa mwisho wa Nkana katika Ligi ya Mabingwa Afrika na ukawa mwanzo mpya kwa Simba katika michuano hiyo. Jana ndiyo droo ilitarajiwa kupangwa mjini Cairo, Misri. Timu zilizofuzu hatua hiyo ni Al Ahly ya Misri, TP Mazembe (Congo DR), Wydad AC (Morocco), Mamelodi Sundowns na Orlando Pirates (Afrika Kusini).AS Vita Club (Congo DR), CS Constantine na JS Saoura (Algeria), Ismaily SC (Misri), Lobi Stars (Nigeria), FC Platinum (Zimbabwe), Horoya SC (Guinea), CA African (Tunisia), Asec Mimosas (Ivory Coast) hizi ndiyo timu zinazotarajia kuumana na Simba katika makundi. Hakuna timu ya kubeza hapo. Hakuna timu nyepesi, wote hawa ni wazoefu na wamejipanga kila kona kuhakikisha wanafanikiwa kutwaa ‘ndoo’.Hiki ni kipimo halisi cha Simba yenye malengo na inayojitutumua kuandika kwa wino mwekundu jina lake katika ramani ya soka la Afrika. Inawezekana popote na muda wowote kama kweli Simba itayavaa mashindano hayo kikamilifu na kuendeleza kile ilichoanza kukifanya tangu katika mechi za awali. Simba hii ina kikosi kipana na chenye kutafuta matokeo kwa machozi, jasho na damu. Inaweza kupambana kwa ajili ya nembo yao kubwa lakini pia ikiiweka begani Tanzania na kudhihirisha Afrika Mashariki sio ya kinyonge! Kila la heri Simba katika mapambano yenu, ni wakati wenu kuudhihirishia ulimwengu wa soka juu ya nini Simba imedhamiria kufanya, inataka kuonesha nini na imepanga kulitawala soka la Afrika. | 4 |
Hayo yalisemwa na Rais wa Bodi ya Ursus, Karol Zarajczyk wakati akitoa maelezo ya kampuni yake mwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipokutana na wafanyabiashara wenye nia ya kuwekeza Tanzania jana kwenye hoteli ya Sheraton jijini Warsaw, Poland.Zarajczyk alisema wanataka kujenga kiwanda hicho nchini Tanzania kwa kutambua nafasi ya kijiografia ya mahali nchi ilipo, kuwa ni fursa ya kufungua milango kwa nchi jirani za Afrika Mashariki na Kati.“Barani Afrika tulianza kupeleka matrekta Ethiopia, Ghana na Guinea. Sasa hivi tumeamua kuja Tanzania na Zambia. Nia yetu siyo kujenga tu kiwanda bali pia kutoa huduma kwa wakulima juu ya uendeshaji na utunzaji wa hayo matrekta,” alisema.Alisema wako tayari kutoa mafunzo kwa vijana wa Tanzania, kama vile chuo fulani ili waweze kuunganisha matrekta hayo hapa nchini na waweze kuyafanyia ukarabati na kutengeneza vipuri vyake pindi ukitokea ulazima wa kufanya hivyo.“Tunapenda kujenga kiwanda mahali ambapo itakuwa rahisi kupata vijana wa kuajiriwa au vijana wa kutoka chuoni ili iwe rahisi kuwafundisha pia teknolojia tunayoitumia kutengeneza matreka hayo,” aliongeza.Kwa upande wake, Waziri Mkuu alisema atawasilisha maelezo yao kwa Waziri anayehusika na sekta hiyo ili mawasiliano rasmi yafanyike. | 5 |
['Manchester United wamepata pigo baada ya mshambuliaji wa Red Bull Salzburg na Norway Erling Braut Haaland, 19, kukubali kujiunga na mabingwa wa Itali Juventus. (Tuttosport, via Express)', 'Arsenal, Newcastle United na Paris St-Germain wameshindwa kumsaini mshambuliaji wa Brazil Everton Soares, 23, kutoka Gremio. (Newcastle Chronicle) ', 'Wolves inakaribia kumsaini mshambuliaji wa Red Bull Salzburg Hwang Hee-chan, kwa dau la £23m baada ya makubaliana na kumsaini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 raia wa Korea Kusini . (Hamburger Morgenpost, via Birmingham Mail)', 'Kazi ya mkufunzi wa West Ham Manuel Pellegrini ipo hatarini na kwamba aliyekuwa mkufunzi wa zamani wa West Ham David Moyes anapigiwa upatu kumrithi.. (Telegraph)', 'Moyes atakubali kurudi kuifunza West Ham iwapo atakabiliwa mikoba ya kuifunza klabu hiyo kwa mkataba wa kudumu.. (Times - subscription required)', 'Mkufunzi wa Everton Carlo Ancelotti anafikiria kurudi katika klabu yake ya zamanai ili kuweza kumsaini kiungo wa kati Lorenzo Insigne, 28. (Le10 Sport, via Star)', "Winga wa Chelsea mwenye umri wa miaka 32 na raia wa Uhispania Pedro, ambaye amekuwa akicheza kama mchezaji wa akiba katika klabu hiyo msimu huu anataka kurudi katika klabu yake ya zamani Barcelona.(L'Esportiu, via Mail) ", 'Manchester United na Paris St-Germain wanampigania beki wa kulia wa Leicester City Ricardo Pereira lakini watalazimika kusubiri hadi mwisho wa msimu huu ili kufanya makubaliano yoyote na nchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 raia wa. (Le10 Sport, via Star)', 'Watford wamekataa ombi la klabu ya Ufaransa ya Lyon kumsaini kiungo wa kati wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 31 Etienne Capoue. (HITC)', 'Arsenal wamehusishwa na uhamisho wa beki wa kati wa RB Leipzig Dayot Upamecano na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 anaweza kuruhusiwa kuondoka katika klabu hiyo ya Ujerumani iwapo klabu hiyo itamsaini mchezaji wa Ufaransa Tanguy Kouassi, 17, kutoka klabu ya Paris St-Germain. (Le Parisien, via Mirror)', 'Klabu ya Hertha Berlin ina matumaini ya kumsaini kiungo wa kati wa Arsenal Granit Xhaka, 27, mwisho wa wiki ijayo. (Daily Mail)', 'Klabu za Burnley na Brighton zinafikiria kumsaini beki wa Hamilton Jamie Hamilton, huku klabu hiyo ya Uskochi ikitaka kulipwa dau la £1.5m kumuuza kinda huyo mwenye umri wa miaka 17.. (Mail)', 'Mkufunzi wa Sheffield United Chris Wilder anataka kuongeza kandarasi ya beki wa Ireland John Egan, 27, na Enda Stevens, 29, pamoja na kiungo wa kati wa England John Lundstram, 25. (Sheffield Star)', 'Chelsea inamtaka winga a PSG na Julian Draxler, 26, na kiungo wa kati wa Senegal mwenye umri wa miaka 30 Idrissa Gueye. (Star)', 'Ajenti wa kiungo wa kati wa Arsenal Xhaka nasema kwamba mchezaji huuyo mwenye umri wa miaka 27 raia wa Uswizi amekubali uhamisho wa kuelekea katika klabu ya Ujerumani ya Hertha Berlin. (Blick, via Mirror)', 'Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta anataka kumsaini kiungo wa kati wa Adrien Rabiot, 24, kwa mkopo kutoka klabu ya ligi ya Seria A Juventus imwezi Januari. (Times - subscription required)', 'Pia unaweza kusoma:', 'Mkufunzi wa Chelsea Frank Lampard anasema kwamba winga wa Brazil Willian 31 ameanza mazungumzo na klabu hiyo kuhusu kuongeza kandarasi yake ambayo inakamilika mwisho wa msimu huu.. (Mail)', 'Bayer Leverkusen itazuia jaribio lolote la Arsenal la kujaribu kumsaini winga wa Ujerumani Kevin Volland, 27, kutoka kwao. (Mail) ', 'Winga wa Manchester City Leroy Sane, 23, atasalia katika klabu hiyo hadi mwisho wa msimu huu lakini raia huyo wa Ujerumani anatarajiwa kuhamia Bayern Munich katika dau la £85m mwisho wa msimu huu . (Star)', 'Man City inachunguza hali ya beki wa Villareal Pau Torres, 22, pamoja na beki wa Portugal Ruben Dias, 22. (Telegraph)', 'Kiungo wa kati wa Dinamo Zagreb na Uhispania Dani Olmo, 21,wamehusishwa na uhamisho wa Manchester City na Manchester United na anasema anataka kuchukua hatua nyengine katika kazi yake.. (Manchester Evening News)', 'Mkufunzi wa Crystal Palace Roy Hodgson anasema kwamba anataka kuwasajili wachezaji wanne au watano katika dirisha dogo la uhamisho la mwezi Januari. (Mail)', 'Babake kiungo wa kati wa Arsenal Mohamed Elneny anasema kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 raia wa Misri ambaye yuko katika klabu ya besikitasa kwa mkopo ameanza mazungumzo kuhusu uhamisho wa kuelekea AC Milan. (Express)', 'Mshambuliaji wa Real Madrid Eden Hazard, 28, huenda akaendelea kuuguza jeraha hadi mwezi januari ama mwanzo wa Februari baada ya raia huyo wa Ubelgiji kupata jeraha hilo mwisho wa mwezi Novemba. (Marca)', 'Kiungo wa kati wa Real Madrid Martin Odegaard, abaye alijiunga na Real Sociedad kwa mkopo kwa miaka miwili anatarajiwa kuitwa na klabu hiyo ya Bernabeu mwezi 2020. (AS)', 'Barcelona itajaribu kumsaini mshambuliaji wa Paris St-Germain na Brazil Neymar, 27, katika dirisha dogo la mwezi Januari. (Goal)', 'Chelsea inafikiria uhamisho wa mwezi Januari wa mshambuliaji wa RB Leipzig na Ujerumani Timo Werner, 23. (Express)', 'Kiungo wa kati wa Man United Paul Pogba, 26, anataka kuondoka katika klabu hiyo na kurudi katika klabu yake ya zamani Juventus. (Calicomercato - in Italian)', 'Mario Mandzukic amemaliza uvumi uliokuwa ukienea baada ya kukamilisha uhamisho wake katika klabu ya Qatari ya Al-Duhail licha ya Man United kuonyesha hamu ya kumsajili kutoka Manchester United. (Mail)', 'Manchester United inajiandaa kumpatia mshambuliaji wa Norway Erling Haaland mshahara wa £200,000 kwa wiki ili kujiunga nao kutoka Red Bull Salzburg. (Sun)', 'Beki wa Chelsea na Uhispania Marcos Alonso, 28, analengwa na klabu ya Inter Milan. (Calciomercato)', 'Mshambuliaji wa Paris St-Germain na Uruguay Edinson Cavani, 32, anakaribia kukamilisha uhamisho wa mwezi Januari kuelekea Atletico Madrid. (Marca)', 'Arsenal inatarajiwa kumuuza mmoja ya washambuliaji wake na kumnunua mshambuliaji wa Lyon na Ufaransa Moussa Dembele. (Le10Sport - in French)', 'Everton na Atletico Madrid wanapigania kumsaini mshambuliaji wa River Plate na Colombia Rafael Santos Borre, 24. (AS)', 'Beki wa Manchester United Chris Smalling, 30, anataka kusalia Roma wakati makubaliano yake ya mkopo yatakapokamilika mwisho wa msimu huu. (Roma Press)', 'AC Milan ina matumaini ya kuafikia makubaliano ya kumsaini mshambuliaji wa Sweden Zlatan Ibrahimovic, 38, katika klabu hiyo mwezi Januari. (Mail)', 'West Ham inafikiria kumsaini beki wakati wa Uhispania Unai Nunez, 22, kutoka Athletic Bilbao. (AS in Spanish)', 'Juan Sebastian Veron anasema kwamba kuna mazungumzo kati ya Estudiantes na kiungo wa kati wa Vissel Kobe Andres Iniesta kuhusu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 wa Uhispania kujiunga na klabu hiyo ya Argentine . (La Oral Deportivo, via Marca)', 'Mkufunzi wa Wolves Nuno Espirito Santo amewapatia wachezaji wake likizo ya siku ya Krismasi kwenda kujumuika na familia zao kabla ya mechi ya siku ya Ijumaa dhidi ya Man. (FourFourTwo)', 'Real Madrid wamemwambia ajenti wa Paul Pogba Mino Raiola kwamba hawatomsaini kiungo huyo wa kati mwezi Januari.. (Mail)', 'Chelsea wamepewa fursa ya kumsaini Isco mwenye umri wa miaka 27 kwa dau la £44m na Real Madrid, hatua itakayotoa fursa kwa mabingwa hao wa Uhispania kumnunua kiungo wa kati wa Tottenham Christian. (Mirror)', 'Beki wa Arsenal na Bosnia-Herzegovina Sead Kolasinac, 26, analengwa na Napoli pamoja na Roma. (Sky Sports)', "Mkufunzi mkuu wa RB Leipzig Oliver Mintzlaff amefichua kwamba wanapata shida kushindana na Manchester United katika kinyang'anyiro cha kumsaini mshambuliaji wa Norway Erling Haaland kutoka Salzburg. (Mail)", 'Tottenham watahitaji kulipa dau la £50m kumsaini beki wa Ufaransa Issa Diop mwenye umi wa miaka ,22, kutoka West Ham. (Express)', "Spurs inafikiria kumsajili kiungo wa kati wa Lille Boubakary Soumare . Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 pia analengwa na Manchester United. (L'Equipe - via Football 365)", 'Borussia Dortmund haitazuia uuzaji wa winga wa England Jadon Sancho, 19, mwezi Januari. (Bild)', 'AC Milan wameweka dau la £26m kwa kiungo wake wa kati Franck Kessie, huku Wolves ikifikiria kumsaini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 mwezi Januari.. (Calciomercato - in Italian)', "Lyon inamnyatia kiungo wa kati wa Atletico Madrid na Ufaransa Thomas Lemar, 24,. (L'Equipe - in French)", 'Atletico wameafikia makubaliano ya kumsaini mshambuliaji wa PSG na Uruguay Edinson Cavani, 32. (Star)', 'Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameungwa mkono kumsajili mshambuliaji wa Juventus na Croatia Mario Mandzukic, 33, kwa makubaliano ya muda mfupi. (Express)', 'Everton wameshauriwa kumsaini mshambuliaji wa Wolves na Mexico Raul Jimenez, 28, pamoja na mshambuliaji wa Southampton Danny Ings, 27. (Talksport - via Star)', 'Mkufunzi wa Leicester City Brendan Rodgers anasema beki wa Croatia Filip Benkovic, 23, huenda akaondoka kwa mkopo mwezi Januari huku klabu ya Derby County. (Leicester Mercury', 'Leeds United inajaribu kuishawishi Arsenal kutomrudisha mshambuliaji wake anayeichezea timu isiozidi wachezaji wa umri wa miaka 21 nchini Uingereza Nketia'] | 4 |
Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye aliwaambia hayo waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumzia ripoti ya sasa ya Benki ya Dunia inayoionesha Tanzania kuporomoka kwa nafasi 11.Sasa Tanzania ni ya 145 duniani na ya mwisho katika ukanda huu wa Afrika ya Mashariki. “Serikali haina budi kuongeza kasi ya kujenga mazingira bora ya biashara ili kuvutia uwekezaji,” alisema.Alisema Serikali inawajibu wa kuweka mazingira bora ya ufanyaji biashara ili nchi isizidi kuporomoka kwenye viashiria vya kimataifa. Alisema katika kukabili hali hiyo watendaji wa Serikali wanatakiwa kufanya kazi kwa vitendo sababu mazingira bora ya biashara ndiyo yanavutia uwekezaji na kukuza pato la Taifa.Alisema taasisi yao imeshitushwa na Tanzania kuporomoka katika uwekaji wa mazingira bora ya biashara na hiyo inaonesha watendaji wa Serikali wanashindwa kutimiza wajibu wao.Ripoti hiyo ya Benki ya Dunia inaonesha Tanzania imeporomoka kutoka nafasi ya 134 mwaka 2013 hadi nafasi ya 145 kati ya nchi 185 katika kuweka mazingira bora ya biashara ili kuvutia uwekezaji.Alisema ripoti hiyo inayotolewa kila mwaka na benki hiyo inaonesha kuwa Tanzania inazidi kushuka kwa miaka mitatu mfululizo.“Ripoti hii imeishitua taasisi yetu na imetusikitisha sana kwa sababu badala ya kupanda tunashuka...na safari hii tumeshuka kwa nafasi 11 hali ambayo si nzuri kwa uchumi wa nchi,” alisema.Benki hiyo inapima hali ya nchi ya ufanyaji biashara kwa kuangalia viashiria vilivyowekwa kimataifa vikiwemo utoaji wa vibali vya ujenzi. | 5 |
SERIKALI imesema itakodi ndege kupeleka matunda na mbogamboga nje ya nchi kutoka katika viwanja vya ndege vya Songwe na Mwanza, wakati huu ikijiandaa kununua ndege ya mizigo kwa kazi hiyo.Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe alisema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema). Katika swali lake, Selasini alisema Mkoa wa Kilimanjaro na hasa Wilaya ya Rombo ni wakulima wazuri wa parachichi, lakini matunda hayo yanapelekwa kwa wingi nchi jirani ya Kenya na kusafirishwa kwenda ughaibuni, kwa nini serikali isinunue ndege ya mizigo kwa kazi hiyo.Kamwelwe alisema kwa sasa serikali inaitumia ndege ya KLM kwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kubeba mazao hayo kila siku kwenda Ulaya. Alisema kutokana na hali hiyo kwa sasa serikali itatumia kukodi ndege katika viwanja vya Mwanza na Songwe kwa ajili ya kubeba minofu na mazao kama parachichi kupeleka Ulaya.Alisema soko la bidhaa kutoka Tanzania kwenda Ulaya ni kubwa, lakini la kutoka Ulaya kuja Tanzania bado ni dogo, hivyo wataendelea kukodi wakati mpango wa kununua ndege ya mizigo ukiendelea kufanyiwa kazi.Akijibu swali la nyongeza, Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alisema hivi sasa serikali inaandaa sheria ya kuunda mamlaka ya kusimamia mazao ya mbogamboga na matunda ambayo itafanya kazi ya kusimamia sekta hiyo yakiwamo mazao ya parachichi. Alisema sheria itatungwa hivi karibuni ya kuwa na mamlaka hiyo, na kwa sasa baadhi ya matunda hayo yanasafirishwa kwa njia za anga na bandari kwenda nje. | 3 |
Ales Mbilinyi – JKCI TAFITI saba za magonjwa ya moyo
zilizofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), zinatarajiwa
kuwasilishwa katika mkutano wa
wanasayansi, madaktari bingwa na wahudumu wa afya wanaotoka nchi za ukanda wa
Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika utakaofanyika wiki ijayo nchini Zambia. Tafiti hizo ambazo zimefanyika
mwaka jana na mwaka huu, ni kuhusu mwenendo wa mapigo ya moyo kwa mgonjwa,
wagonjwa wenye moyo ambao uwezo wake wa kufanya kazi umepungua jinsi wanavyozingatia matibabu kama
walivyoshauriwa na madaktari, shinikizo la damu na tatizo la kisukari. Nyingine ni upungufu wa nguvu za
kiume katika jamii, uelewa wa sababu hatarishi za magonjwa ya moyo katika
jamii, magonjwa matatu kwa pamoja yaani
moyo na figo kushindwa kufanya kazi na
upungufu wa damu mwilini. Akizungumza kuhusu tafiti hizo,
Mkuu wa Kitengo cha Utafiti wa JKCI, Dk. Pedro Pallangyo, alisema tafiti hizo
zimefanyika Mkoa wa Dar es Salaam kwa kipindi cha miaka miwili na kwa wagonjwa
wanaotibiwa katika taasisi hiyo. “Tumekuwa tukifanya tafiti mbalimbali kuhusu
magonjwa ya moyo ambazo zinatusaidia kufahamu wagonjwa wetu pamoja na wananchi
wanaotuzunguka wanakabiliwa na matatizo gani katika afya za moyo na hii inatusaidia
kuweza kuboresha huduma zetu,” alisema. Kuhusu mkutano huo wa magonjwa
yasiyo ya kuambukiza, Dk. Pedro alisema kwa upande wa magonjwa ya moyo
utawasaidia kubadilishana matokeo ya
huduma za matibabu wanazozitoa, hasa tafiti zinazofanywa katika nchi
mbalimbali ili kuboresha huduma
zinazotolewa kwa wagonjwa. Ofisa Uuguzi wa JKCI, Jalack
Milinga, ambaye alishiriki kufanya tafiti hizo, alisema kwake ni mara ya kwanza kuhudhuria mkutano
huo ambao utamsaidia kuongeza ujuzi katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa
moyo, lakini pia kubadilishana uzoefu na wauguzi wenzake watakaoshiriki. “Utafiti wangu uliangalia jinsi ya
uzingatiaji wa unywaji wa dawa za moyo kwa wagonjwa ambao mioyo yao haifanyi
kazi vizuri. “Hivyo naamini ushiriki wangu
katika mkutano huu utaniwezesha kupata mbinu mpya za kusimamia jukumu
la kuwasaidia wagonjwa wetu kuzingatia matibabu ili kupata matokeo bora
ya tiba,” alisema Milinga. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo
wa JKCI, Smita Bhalia, alisema ushiriki wa wataalamu kutoka Tanzania umelenga kutoa matokeo ya utafiti uliofanywa
hapa nchini na kuonyesha baadhi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza jinsi
yanavyoweza kusababisha magonjwa ya moyo ama magonjwa ya moyo yanavyoweza kusababisha
mtu kupata magonjwa mengine yasiyo ya kuambukiza. Malengo ya mkutano huo ni kwa
nchi washiriki kutoka ukanda wa Mashariki, Kati na Kusini mwa
Afrika kuona jinsi ya kushirikiana
katika kufanya tafiti za ndani, kuwa na
njia bora na za kisasa za matibabu ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza na kuwa na
mbinu mpya za kuweza kuzuia magonjwa hayo. Mkutano huo ambao hufanyika kila
mwaka, unatarajia kufayika mjini Livingstone, Zambia kuanzia Septemba 5 hadi 7.
Mwaka jana ulifanyika Nairobi nchini Kenya. | 3 |
Brighiter Masaki, Dar es Salaam Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wamiliki wa nyumba jijini humo kuwapunguzia kodi ya miezi mitatu wapangaji wao kwa asilimia 50 kutokana na hali ya uchumi ilivyo katika kipindi hiki cha mlipuko wa janga la virusi vya corona. Makonda ametoa kauli hiyo leo Jumatano Aprili Mosi, alipokuwa akizungumza na wananchi katika kituo cha mabasi cha Makumbusho jijini Dar es Salaam. “Nimeongea na wenye nyumba na kuwataka wapunguza kodi kwa asilimia 50 ili kusaidia kufanya biashara na kuangalia hali ya uchumi ilivyo kwa sasa kama mnavyofahamu corona imeathiri hali ya kifedha,” amesema Makonda. Aidha amewaruhusu waendesha pikipiki maarufu bodaboda, kuingia mjini ili kupunguza adha ya usafiri na msongamano katika vituo vya daladala baada ya kutangazwa utaratibu mpya wa ‘level seat’ ili kuepuka maambukizi ya virusi hivyo. “Tunachotakiwa kufanya hivi sasa ni kusaidia wafanyakazi kuwahi kazini na kufanya shughuli kwa wakati ili tuweze kuepukana na hali ngumu ya maisha,” amesema Makonda. Pamoja na mambo mengine, Makonda ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu (Sumatra), kuhakikisha ifikapo kesho jumatano Aprili 2, saa 6:00 mchana wawe wameshabadilisha ruti za magari kuwa fupi. | 0 |
CHRISTINA GAULUHANGA -DAR ES SALAAM JAMII imeshauriwa kuepuka matumizi ya dawa za kulevya kwakuwa zina madhara mengi ikiwamo wanawake watumiaji kuharibu mfumo wa hedhi na kuharibika kwa mimba. Akizungumza na MTANZANIA jana jijini Dar es Salaam katika Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa, Ofisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Makosa ya Jinsi nchini Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Ched Ngagunga alisema katika maonyesho hayo wameyatumia kutoa elimu alimu ya athari za dawa za kulevya na mbinu rahisi za Kudhibiti matumizi ya dawa hizo kuanzia ngazi ya familia. Alisema katika maonyesho hayo zipo dawa za aina mbili za viwandani na mashambani ambapo nyingine inasisimua misuli na nyingine inafanya mtumiaji kuzubaa au kusinzia. Alisema madhara ya matumizi ya dawa hizo za Kokeini na Heroini ni makubwa na yanafanana ambapo wengi wanapenda kutumia Heroini kwa kuwa inapatikana kwa bei nafuu. “Matumizi ya dawa hizi yana madhara makubwa kwa wanawake kwani yanaharibu mfumo wa uzazi, mimba pia kwa wanaume wengi wanakosa hamu ya tendo la ndoa na hata wanaopenda tendo na hata anayeitumia kokeini anapenda ngono mara kwa mara japokuwa inakuwa haina nguvu,” alisema Ngatunga. Alisema Kokeini nyingi zimekuwa zinatoka ukanda wa Amerika Kusini yaani Brazil, Mexico, Peru, Colombia na kwingineko. Alisema watumiaji wa dawa hizo wengi huwa wachangamfu kupita kiasi halafu wanakuwa na ndoto ambazo hazipo pia wanaangaalia kwa kutanua sana mbinu ya hicho. Ngatunga alisema pia kwa mtumiaji wa mirungi ni rahisi kupata vidonda vya tumbo, sarani ya koo, meno kuoza, kuharibu figo, kukosa hamu ya kula, kushindwa kufanya tendo la ndoa na kukosa usingizi. Ngatunga alitoa tahadhari kwa jamii pindi wanapokuja safari kutokubali kupewa chakula cha aina yeyote ikiwamo keki, madhara au vinywaji. | 0 |
GRACE SHITUNDU -DAR ES SALAAM MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, amevitaka vyama vinavyohofia kufutwa kutokana na uhakiki wa vyama unaotarajiwa kufanywa na ofisi hiyo kuanzia Machi 17, viondoe hofu kwani lengo ni kuondoa vyama vya mfukoni. Akizungumza na viongozi wa vyama hivyo Dar es Salaam jana, Jaji Mutungi alisema lengo la uhakiki huo ni kufanya tathmini ya vyama ili kuondokana na dhana ya kuwepo chama cha mfukoni. “Kazi ya uhakiki ni moja ya majukumu yanayofanywa na ofisi ya msajili na kazi ya chama ni kutunza uhalali wake, kuhakikisha kinakuwa hai, hivyo tunapofanya uhakiki ni kujiridhisha. “Zoezi hili halina nia ya kutaka kufuta chama chochote, bali ni kufanya tathmini na kuangalia endapo vyama vilivyopo vina vigezo vyote vinavyohitajika,” alisema Jaji Mutungi. Akizungumza lengo la kikao hicho, Jaji Mutungi alisema ni kuwajulisha mapema zaidi kuhusu uhakiki huo. “Tunachojaribu kuwaeleza hapa ni kuwaweka tayari, isiwe kama dereva wa daladala akimuona askari ndio anafunga mkanda akiondoka anafungua, tunataka kuwasaidia ninyi muwe na mahali pazuri pa kufanyia kazi zenu za chama,” alisema Jaji Mutungi. Alisema ofisi yake inataka vyama hivyo vijiendeshe kama taasisi kamili. “Tunataka vyama vya siasa vijiendeshe kama taasisi, kuna wakati wenyewe kwa wenyewe mnakosana, basi mmoja wenu anafunga ofisi na nyaraka muhimu za chama unakuta zipo ndani, shughuli zote za chama zinasimama,” alisema Jaji Mutungi. Naye Naibu Msajili vya Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza, alisema katika zoezi hilo watapita kufanya uhakiki katika ofisi zote za makao makuu ya chama na ofisi ndogo, Bara na Visiwani. “Zoezi la uhakiki limepangwa kuanza Machi 17 mwaka huu na tutapita katika ofisi zote za vyama, makao makuu na ofisi ndogo, chama chochote cha siasa kinapaswa kuwa na ofisi kuu na ndogo hapa Tanzania Bara na Visiwani,” alisema Nyahoza. Alisema uhakiki huo hautaishia katika ofisi kuu pekee, bali utaendelea kwenye ofisi za mikoa na wilaya. “Uhakiki wetu hautaishia katika ofisi kuu peke yake, kuna siku tutaamua kwenda mkoani kuangalia kama chama chenu kipo, kwani ni lazima chama kiwe na orodha ya wanachama katika ngazi mbalimbali mkoa, wilaya au jimbo,” alisema Nyahoza. Akizungumzia mambo mengine watakayofanyia uhakiki ni pamoja na kuangalia orodha ya mali na vifaa vya chama. “Rejista ya samani au mali za chama, kitu chochote cha chama kisajiliwe kwa jina la chama, kwani inawezekana mtu akanunua kochi kwa ajili ya ofisi, mwisho wa siku wakikorofishana anaanza kudai ofisi kochi lake,” alisema Nyahoza. Pia alisema kuhakikisha chama kinakuwa na akaunti maalumu ambayo fedha zinapitia huko ili kuweka kumbukumbu ya mapato na matumizi. “Kwa vile vyama ambavyo vinapokea ruzuku vinatakiwa kuwa na akaunti mbili ambapo fedha za ruzuku zisichanganywe na zile zinazotokana na vyanzo vingine ili kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa mambo yanayohusu fedha ya ruzuku tu,” aliongeza Nyahoza. | 3 |
NA JUDITH PETER, DAR ES SALAAM INATIA shaka! Ndivyo unavyoweza kuielezea hatima ya mshambuliaji Msenegali, Papa Niang kusajiliwa na timu ya Simba, kufuatia kuonyesha kiwango kisichoridhisha kwenye mchezo wake wa kwanza ndani ya timu hiyo dhidi ya Mwadui katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam jana. Niang aliyewasili nchini Ijumaa iliyopita kusaka ulaji wa kusajiliwa na Simba inayosaka straika hatari wa kufumania nyavu, alicheza kwa dakika 45 tu za kwanza za mchezo huo kabla ya kutolewa kipindi cha pili. Lakini alionekana kutokuwa fiti mchezoni kuanzia kukimbia hata namna ya kupambana uwanjani, hali iliyowafanya baadhi ya mashabiki wa Simba nao kupata shaka juu ya uwezo wake na kuanza kumponda wakidai bado sana. MTANZANIA lilifanya jitihada za kumpata Kocha wa viungo wa Simba, Dusan Momcilovic raia wa Serbia baada ya Kocha Mkuu Dylan Kerr kupotea, ambaye alisema kwa ufupi kuwa: “Bado hayupo fiti, hawezi kuwa straika, kukimbia hawezi sidhani kama anaweza kuisaidia Simba, hata kutolewa kwake ilikuwa kwa sababu hiyo. Ila atapewa programu maalumu.” Moja ya kosa kosa alizofanya Niang kwenye mchezo huo ni dakika ya 5 alipokuwa akitazamana na kipa wa Mwadui, Shabani Kado, lakini beki Joram Mgeveke alimzidi ujanja na kuondoa hatari hiyo. Simba ilionekana ikicheza bila mipango yoyote ya kusaka bao, eneo lake la ushambuliaji likionekana kupwaya kwa wachezaji kutoelewana vema. Kocha wa Simba, Dylan Kerr, alianza kwa kuwaanzisha Mwinyi Kazimoto, Awadh Juma na Mzimbabwe, Justice Majabvi, huku kwenye ushambuliaji Niang akicheza sambamba na Mussa Hassan ‘Mgosi’. Hata baada ya kipindi cha pili Kerr kuwapumzisha Niang na Mgosi na kuwaingiza Hamis Kiiza na Danny Lyanga, bado Simba iliendelea kukosa mabao. Kiiza mwenyewe akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga dakika ya 58 alipiga shuti dogo lililodakwa vema na Kado, ambaye aliumia dakika ya 77 kwa kugongana na Lyanga wakati akiwa kwenye harakati za kuokoa shambulizi la Simba, nafasi yake ilichukuliwa na Jackson Abdulazak. Katika mchezo huo, Simba iliweza kuwatumia makipa wake wote watatu, Muivory Coast, Vincent Angban aliyetoka dakika ya 30 na kuingia kinda Denis Richard, ambaye naye alipumzishwa dakika ya 64 na kuingia Manyika Peter Jr. Wachezaji wapya wa Mwadui waliocheza Ligi Kuu msimu uliopita, Jerryson Tegete na Nizar Khalfan (wote Yanga) na Paul Nonga (Mbeya City), walioingizwa kipindi cha pili nao walishindwa kuisadia timu hiyo iliyopanda daraja na kutoa sare hiyo. Hiyo ni sare ya kwanza kwa kocha Kerr tangu aanze kuinoa Simba, kati ya mechi nane za kirafiki alizoiongoza, saba ameibuka na ushindi wa asilimia 100 huku timu hiyo ikifunga mabao 18. | 4 |
Serikali ya Misri kupitia Wizara ya Nishati imetangaza fursa kwa Watanzania 50 kwenda nchini humo kwa ajili ya mafunzo mbalimbali yahusuyo nishati.Akizungumza leo (Julai, 26, 2019) kabla ya tukio la kuweka jiwe la msingi katika mradi wa umeme Rufiji, Waziri wa Nishati wa Misri, Dk Mohamed Shaker amesema kuwa serikali hiyo ilikuwa imepanga kutoa nafasi 20 tu lakini kwa sasa imeongeza hadi kufikia 50.Vilevile, Waziri huyo ameongeza kuwa lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwaandaa Watanzania watakaokuwa na uwezo na ufanisi wa kusimamia miradi hiyo, sambamba na kuandaa wigo mpana wa kupata ajira katika mradi huo unaotarajiwa kuzalisha zaidi ya Megawati 2,000.Mradi wa Umeme wa Rufiji, ambao Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi leo, unajengwa kwa ubia wa wakandarasi; Arab Contractors na Elsewedy zote za Misri.Hadi kukamilika mnamo 2022, mradi huo unatarajiwa kugharimu Sh trilioni 6.6 hadi kukamilika kwake.Viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na wawakilishi wa taasisi za kimataifa, mabalozi na wananchi takribani 2000 wamehudhuria sherehe hizo. | 3 |
Na KULWA MZEE-DAR ES SALAAM MSAMAHA
uliotolewa kwa watuhumiwa wa kesi za uhujumu uchumi na kutakatisha fedha
unaonekana kugubikwa na changamoto zinazopunguza kasi ya utekelezaji wake. Wakati
siku saba nyingine ukiacha zile za mwanzo zilizotolewa na Rais Dk. John
Magufuli zikielekea kufikia ukingoni Jumatano, imebainika kuwa miongoni
washtakiwa wengi wameandika ‘barua kuomba msamaha’ na si ‘barua za kuomba msamaha
na kukiri makosa yao na kurejesha fedha’. Ushauri
alioutoa Rais Magufuli kwa Mkurugenzi wa Mashataka nchini (DPP), Biswalo Mganga
unaelekeza watuhumiwa hao kuandika barua kukiri makosa yao na kuomba msamaha na kisha kurejesha kiasi
cha fedha wanachodaiwa. Kinachothibitisha
kuwapo kwa hali hiyo ni kutokana na yale
yaliyojitokeza juzi Ijumaa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambako utekelezaji wa msamaha huo ulikwama kwa watuhumiwa takribani 50 waliotoka
katika Gereza la Segerea na Keko. Miongoni
mwa watuhumiwa hao na wale waliofikishwa kabla baadhi walibainika kuomba
msamaha pasipo kukiri makosa yao. Hali
hiyo ni kama aliiona mwanzo Rais magufuli mwenyewe baada ya utekelezaji wa
ushauri wa siku saba alizozitoa mwanzo. Wakati
DPP akimkabidhi taarifa ya utekelezaji wa ushauri huo Septemba 22 mwaka huu,
Rais Magufuli alisema wapo watuhumiwa
wanaodanganywa kwamba msamaha huo ni wa uongo na kwamba mtuhumiwa anakuwa
amejishtaki mwenyewe. Rais
Magufuli aliwataka watuhumiwa hao wasiamini maneno hayo kwa kuwa msamaha
ukitolewa lazima uwe msamaha. MTANZANIA
Jumapili limebaini kuwa baadhi ya watuhumiwa bado wanahofu hiyo na ndiyo msingi
wa kuandika barua za kuomba msamaha pasipo kukiri makosa yao kwa kuwa wanaamini
rekodi zao zinaweza kuwahukumu. Mfano
wa watuhumiwa hao ni raia wa China, Cheng Guo anayeshtakiwa kwa kusafirisha
nyara za Serikali aliyechafua hali ya hewa baada ya kukana kuandika barua ya
kuomba msamaha na kukiri makosa ya kusafirisha nyara hizo zenye thamani ya Sh
267,407,400. Mshtakiwa
huyo anayedaiwa kusafirisha meno ya tembo na kucha za Simba alikuwa miongoni
mwa washtakiwa wengi waliotolewa gerezani kuletwa mahakamani kwa ajili ya
kukiri makosa kutokana na barua walizoandika. Wakili
wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon aliiwakilisha Jamhuri mbele ya Hakimu
Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alidai mshtakiwa aliandika barua ya kuomba msamaha. “Uliandika
barua ya kukiri makosa? alihoji Hakimu Shaidi. Mshtakiwa
alijibu hapana, hakuandika barua ya kukiri makosa, yeye aliandika barua ya
kulalamika upelelezi kuchelewa na kuomba msamaha. “Sijaandika
barua ya kukiri makosa, sina hela za kulipa,”alidai. Jambo
jingine linalowatia hofu baadhi ya watuhumiwa, ni kutojua kile kitakachoamriwa
mbele ya mahakama baada ya kukiri na kuomba msamaha na kwa kuzingatia pia
kwamba Rais Magufuli mwenyewe na hata DPP wamesisitiza mchakato huo lazima
umalizike kupitia mahakamani walikoingilia. Aidha
kauli ya DPP wakati akitoa taarifa ya utekelezaji kwamba mtu mmoja aliyekubali kuitikia wito huo baada
ya kukiri kosa mahakamani na kulipa Sh bil 1.4 moja kwa moja lakini bado Mahakama
ikamtoza faini ya sh milioni tano kutokana na kukiri kosa ndiyo ambayo baadhi
ya watuhumiwa wanaona inawafanya washindwe kubashiri kile ambacho mahakama nayo itaamua baada ya
kukiri makosa yao. Hoja
ya kutojipanga kwa ajili ya kutekeleza masharti ya msamaha huo nayo imeonekana
kujitokeza kwa baadhi ya watuhumiwa waliofikishwa mahakamani hapo. Baadhi
ya washtakiwa wamesema hawakuwa wamefanya mawasiliano na ndugu zao kwa ajili ya
kukamilisha urejeshaji wa fedha walizokiri kulipa. Mahabusu
wengi waliokuwa wakipanda kizimbani walikuwa wakilalamika kwamba wengine ndugu
zao wako mikoani hawana taarifa pamoja na kwamba waliandika barua. Miongoni
mwa washtakiwa ambao hawakupata muda wa kujipanga kwa utekelezaji ni Michael
Wambura ambaye aliweka wazi mahakamani kwamba hakuwa ameweka mambo yake
sawasawa. Katika
barua yake kwa kujua kwamba kosa la kutakatisha adhabu yake ya chini ni faini
Sh milioni 100 alisema hana uwezo wa kuwa na fedha hizo, uwezo wake ni Sh milioni 85 hivyo
anasubiri huruma ya DPP, Jumatatu
akiri na kurejesha kiasi
atakachokubaliwa. Baada
ya Rais John Magufuli kutangaza msamaha huo, DPP amekuwa akipokea barua nyingi
ofisini kwake ambazo ameweza kuzishughulikia na kuyafikisha majalada ya baadhi ya
watuhumiwa hao mahakamani Ijumaa. Wakati
akitoa taarifa ya utekelezaji wa siku saba za mwanzo za msamaha ambapo
watuhumiwa 467 wameandika barua, DPP alisema kuwa wanalazimika kukaa kusoma na
kuchambuan kwa kina majalada ya watuhumiwa waliopokea wito huo ili kuangalia yapi wanakubaliana nayo na yapi ya kurekebisha mashataka na kwenda nayo mahakamani kwa mujibu wa
sheria ili watuhumiwa hao waweze kulipa mahakamani na isitokee katika siku
zijazo wakatumia mbinu nyingine kuishtaki serikali. MAHAKAMA KUZIDIWA Aidha
kutokana na mwitikio wa msamaha huo kuwa mkubwa, kabla na baada ya siku saba za
sasa, kuna uwezekano wa Mahakama kuzidiwa kutokana na muda mchache na barua kuwa nyingi. Siku
ya Ijumaa watuhumiwa walikuwa wengi na kufanya mahakama ifanye kazi hadi muda
wa jioni. Gazeti
hili lilishuhudia baadhi ya kesi zikichukua muda mwingi hasa kwa upande zile
zenye mashtaka mengi. Mshtakiwa
ama washtakiwa wanapoingia mahakamani husomewa upya mashtaka yanayomkabili ama
kuwakabili kulingana na walichokubaliana na DPP. Mshatakiwa
anakiri makosa hayo, anasomewa maelekezo ya awali, kama kuna vielelezo
vinatolewa kisha mahakama inatoa adhabu ya faini kwa mujibu wa sheria na adhabu
ya kifungo endapo atashindwa kulipa faini. Adhabu
ya chini kwa makosa ya kutakatisha fedha ni faini Sh milioni 100 na adhabu ya
juu kwa faini ni Sh milioni 500 . MAHAKIMU Aidha
kutokana na zoezi hilo kuwa ni la muda maalum baadhi ya wadau wa mahakama wanaona
kuna haja ya kuweka utaratibu maalum kwa mahakimu wa kesi husika. Hilo
linatokana na kile kilichotokea Ijumaa kwenye kesi ya vigogo wa NIDA ambao kesi
yao haikuweza kusikilizwa kwa sababu Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salum Ally
hakuwepo. Kwa
sababu hiyo wadau hao wameshauri kuangalia namna nyingine ya kuharakisha
utekelezaji wa ofa hiyo kwa kuyagawa mafaili kwa mahakimu wengine ikitokea muhusika
hayupo vinginevyo mtuhumiwa atakosa kupata haki hiyo ya kusamehewa kama
alivyoomba. Aidha
kwa siku mbili za mwishoni mwa wiki ambazo watuhumiwa walianza kufika kukiri
baada ya barua zao kupitiwa kumeonekana ongezeko kubwa la wananchi wanaofurika
mahakamani kufatilia ndugu na jamaa zao. Ni
mazingira kama hayo pia wadau hao wanaona kuna haja pia kwa Jeshi la Polisi
kuimarisha ulinzi katika mahakama zote ambazo zinatekeleza ofa kwa ajili ya
usalama. | 3 |
Akizungumza na waandishi wa habari jana Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa alisema kuwa katika kikao chake Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imebatilisha uamuzi uliochukuliwa na Kamati ya Saa 72, kutokana na kuwa upungufu mwingi.Kamati ya Saa 72 iliwapa Simba pointi tatu baada ya timu hiyo kukata rufaa ikidai kuwa Kagera Sugar ilimchezesha mchezaji Mohamed Fakhi aliyekuwa na kadi tatu za njano. Alisema, kamati hiyo haikukidhi matakwa yaliyotakiwa ili kusikilizwa kwa hoja za Simba ambapo alitaja masharti hayo kuwa ni kushindwa kulipa ada ya malalamiko ambayo ni Sh 500,000.Simba haikuwakilisha malalamiko yake kwa wakati husika ambao unatakiwa kuzingatiwa pamoja na kushirikishwa kwa wajumbe wasiokuwa na sifa kwenye mkutano huo. “Simba ililalamikia suala lake hilo bila ya kuzingatia taratibu kwa kuwa ilishindwa kuzingatia kanuni sahihi kwa kuwa kanuni ya 20 katika vifungu tofauti kifungu cha kwanza kimeweka wazi kuwa klabu inatakiwa kuwasilisha malalamiko yao ndani ya saa 72 huku kile cha pili kikiweka wazi kuwa ada ni lazima ilipwe yote kwa wakati,” alisema Mwesigwa.Aliongeza: “Hiki kinachowakuta Simba leo (jana) ni sawa na kile kilichoikumba timu ya Polisi ambayo nayo iliilalamikia Simba, lakini haikulipa ada ya kusikilizwa kwa shauri lao”. Pia alisema kuwa kamati hiyo imeitaka bodi ya Ligi kuwafikisha katika kamati ya maadili maofisa wake wawili kwa kosa kimaadili ambapo Katibu huyo hakutaja majina ya maofisa.“Suala la maofisa hawa wa Bodi ya Ligi kwa uzembe au kushindwa kuzingatia maadili ya kazi watatakiwa nao kuwajibishwa na kuhusu suala hilo aulizwe zaidi Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi hiyo,” alisema Mwesigwa. Simba sasa ina pointi 59 baada ya kuchukuliwa pointi hizo wakati Yanga ikiendelea kubaki katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 56 lakini ina mechi mbili mkononi. | 4 |
Ashura Kazinja-Morogoro KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.
Bashiru Ally, amesema ni vyema Serikali ikaona umuhimu wa kutenganisha barabara
za kupita magari ya mizigo na ya kawaida ili kuepusha hatari kwa wananchi. Dk. Bashiru aliyasema hayo jana wakati alipotembelea
majeruhi waliopata ajali ya moto wa lori la mafuta lililoanguka mkoani
Morogoro. Mbali kutembelea majeruhi waliolazwa Hospitali
ya Mkoa wa Morogoro, pia alitembelea chumba cha kuhifadhia maiti, kuomba dua
makaburini na eneo la Itigi-Msamvu ambako lori hilo lilipinduka kabla wananchi
hawajalivamia kuiba mafuta na baadaye moto kulipuka. Alisema kutenganishwa huko kutasaidia
magari makubwa kutopita maeneo ya makazi ya watu na hata kukitokea majanga kama
ya moto, wananchi hawataweza kupata madhara. Hata hivyo, aliishauri Serikali kuweka
utaratibu wa kutoa elimu ya majanga ya moto ili wananchi waweze kuwa na uelewa
mara zote na kuweza kukaa mbali na matukio ya moto ikiwemo yanapoanguka magari
ya mafuta. Akizungumza na wananchi jirani na eneo la tukio
lilipotokea, Dk. Bashiru aliwataka kutokata tamaa baada ya kufiwa na ndugu zao
na watu wao wa karibu ambao ni nguvu kazi ya taifa kwani kifo hupangwa na
Mungu. “Hili ni janga la kitaifa, poleni sana,
kwani wengi wamejeruhiwa na kufa, lengo letu ni kuendelea kuwafariji na
kuangalia changamoto zilizopo ikiwemo upande wa majeruhi kwa ajili ya
kupatikana madawa,” alisema. Alisema Serikali na wananchi hasa vijana
wakiwemo wa CCM wameonyesha ushirikiano mkubwa wa kusaidia mambo mbalimbali,
ikiwemo kupeleka maiti na majeruhi hospitali kutoka eneo la tukio kwa haraka. Aidha aliipongeza Serikali ya awamu ya tano
kwa kuimarisha sekta ya afya na kufanya majeruhi wa ajali hiyo kuishia kutibiwa
kwenye hospitali za ndani badala ya kupelekwa nje ya nchi, na kwamba hiyo ni
hatua kubwa iliyopigwa. SAMPULI 85 ZA DAMU ZACHUKULIWA Kaimu Mkurugenzi idara ya Sayansi, Jinai na
Huduma za Vinasaba, David Elias, alisema tangu tukio limetokea hadi sasa,
wameshachukua sampuli 85 za damu za watu, ili kuwawezesha ndugu kutambua
marehemu wao, au walio majeruhi hospitalini. Elias alisema sampuli hizo zimepelekwa Kitengo
cha Kupima Vinasaba (DNA) Dar es Salaam na kwamba majibu yatatolewa wiki mbili
baada ya kupelekwa kwenye mashine. Alisema wananchi waliochukua miili ya ndugu
zao na kuizika ni wale walioitambua kutokana na alama mbalimbali za miili yao,
na kwamba licha ya kuchukua au kutambua miili hiyo, sampuli zao zimepelekwa
kwenye mashine na majibu yatapatikana. RC ATAKA MAJERUHI WAOMBEWE Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk. Steven Kebwe,
alisema siku ya tukio alilazimika kupanda lori la mawe ili kuwahi kwenye eneo
la tukio baada ya gari lake kuwa katika majukumu mengine. Alisema alijaribu kupiga simu kuita taxi,
lakini ilichukua muda mrefu kufika na hivyo kulazimika kupanda lori. Akizungumzia majeruhi, alisema kiafya
mgonjwa aliyeungua moto kwa asilimia 50 nafasi ya kupona kwake hubaki kuwa ni
asilimia 2, hivyo ni jambo la busara kuzidi kuwaombea majeruhi waliopo
Muhimbili wapone. Alisema majeruhi 16 waliopo Hospitali ya
Rufaa Mkoa wa Morogoro wanaendelea vizuri huku wengine wakiwa na uwezo wa
kujieleza. MAJERUHI ASIMULIA ALIVYOJERUHIWA Mmoja wa majeruhi, Boniphace Steven,
alisema alikuwa akienda kazini kwake Islamic Foundation, na alipofika eneo lori
hilo lilipoanguka, alisimama kushangaa ndipo moto ulipolipuka na yeye kujikuta
miongoni mwa wahanga. MADAWA
NA VIFAA TIBA Kwa
mujibu wa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Morogoro, Dk. Kusirye Ukio, mbali
na kupongeza juhudi za Serikali na wanachi katika michango yao ya hali na mali,
mchango mkubwa unaohitajika zaidi kwa sasa ni madawa na vifaa tiba ili
kuwawezesha madaktari na wauguzi kufanya kazi kwa weledi zaidi. “Tumeona
juhudi za Serikali na wananchi kuunga mkono katika kuchangia zoezi hili, labda
niwakumbushe wasamaria wema kuwa tungependa kupata vitu zaidi kuliko fedha
kwani tuna imani kuwa hiyo ndiyo dhamira ya kupigania uhai wa wagonjwa,”
alisema Dk. Ukio. SHUKURANI
KWA SERIKALI Mwenyekiti
wa Mtaa wa Suma uliopoteza watu 19, Khamisi Totoro, aliishukuru Serikali kwa
juhudi walizoonyesha na kuweza kuwapa ushirikiano toka mwanzo wa tukio hadi
sasa. | 3 |
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi katika hafla ya kumpongeza Samatta iliyoandaliwa na Kampuni ya Propel Global.Alisema tatizo lililopo kwa viongozi wengi huwatumia vijana hao katika mambo yao binafsi na sio kuwasaidia kutimiza ndoto zao.“Mimi ninaamini mkiacha ubinafsi mtapata vijana wengi wenye vipaji, watapata maisha bora na kulitangaza soka la Tanzania,” alisema na kuongeza kuwa viongozi hao hutafuta maisha mgongoni mwa wachezaji.Katika hatua nyingine, Rais wa TFF, Jamal Malinzi aliomba ushirikiano wa serikali katika kutimiza mikakati yao ya kuendeleza soka, lakini pia katika maandalizi ya kuandaa michuano ya vijana ya Afrika chini ya umri wa miaka 17.Akizungumzia ombi hilo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye alisema amelipokea na kuahidi kupitia mikakati ya TFF na kuona ni jinsi gani watashirikiana ili itekelezeke.Pia ombi la TFF kuhusu kuachiwa mashindano ya michezo kwa shule za msingi (Umitashumta) na sekondari (Umisseta) katika mchezo wa mpira wa miguu limeahidiwa kufanyiwa kazi mapema ili kusimamia na mipango yao kufikia mahali pazuri. | 4 |
Na Aziza Masoud ASILIMIA kubwa ya watoto wanaoharibika kitabia huchangiwa na mazingira pamoja na aina ya malezi anayopatiwa na mzazi au mlezi. Wapo baadhi ya watoto wanaharibika kitabia kwa sababu ya mzazi kutokuwa makini, hasa wale wanaofanya shughuli za kujitafutia kipato mbali na maeneo wanayoishi, hivyo wanakosa muda wa kuangalia watoto kwa ukaribu. Wazazi wanaofanya kazi ama shughuli mbali na maeneo ya makazi yao mara nyingi huwaacha watoto wao nyumbani na kulelewa na dada wa kazi na wengine hulelewa na ndugu ambao wanatoka katika familia husika. Hali hii huchangia watoto kujifunza mambo mengi, yakiwamo mazuri na mabaya kulingana na tabia ya mtu anayekuwa naye kwa muda mrefu. Kumekuwa na wimbi kubwa la watoto wa kiume na wa kike ambao wanajiingiza katika vitendo vichafu, ikiwamo kujihusisha na mapenzi wakiwa katika umri mdogo. Jambo hili lina sababu mbili, zipo ambazo zinachangiwa na mtoto husika kuwa mtukutu, lakini sababu nyingine ni uangalizi mbovu wa wazazi. Mazingira ya maisha ya siku hizi mzazi anakuwa na shughuli nyingi zinazomfanya kuondoka nyumbani asubuhi na mapema na kurudi usiku. Mbali na kuwahi kuamka, pia muda wa kurudi nyumbani nao unakuwa si rafiki, kwakuwa wapo ambao hurejea kuanzia saa mbili usiku, hivyo anakuta mtoto akiwa amelala. Ratiba za namna hii zinafanya mzazi kutopata muda wa kutosha wa kukaa na mtoto ili kujadili mambo mbalimbali ambayo mengine yanakuwa yanamfurahisha ama kumkwaza. Kama mzazi ni mtu wa kujishughulisha muda mwingi, ni vizuri ukaanzisha utaratibu wa kutenga muda wa kukaa na mtoto wako kipindi cha mwishoni mwa juma. Hii itakusaidia kumjua mtoto wako jinsi anavyoishi na watu wake na hivyo kumwepusha na makundi ya watoto wenye tabia mbaya ambazo zinaweza kuchangia kumharibu. Kikawaida mtoto ni mtu wa kuongea endapo utamuwekea mazingira ya kuwa karibu naye, wazazi tunapaswa kufahamu kuwa, ukaribu wa mama na motto, hasa nyakati za jioni ni muhimu sana na huenda ukamwokoa mtoto katika kufanya mambo mabaya. Mzazi unapaswa kuwa na ratiba ya kuongea na mtoto kila siku za jioni huku ukimuuliza mambo mbalimbali aliyoyafanya na kuyaona kwa siku nzima. Njia hii inaweza ikamwokoa, kwakuwa watoto wengi hawana ujasiri wa kuficha siri kama anafanyiwa mambo tofauti na aliyoyazoea. Wazazi tunapaswa kufahamu kuwa, dunia imebadilika, mtoto anatunzwa na mzazi husika, si dada wa kazi wala ndugu, tuwe na utaratibu wa kuongea na watoto ili tuwaepushe kuingizwa katika tabia hizi zisizofaa. | 0 |
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Maromboso jijini Arusha,Theresia Sidoyeka ameshindwa kusoma hukumu katika shauri la mirathi iliyokuwa isomwe jana kwa maelezo kuwa hukumu hiyo iliibwa ofi sini kwake.“Jamani hukumu yenu niliyokuwa nimeiandika kwa kuichapa imeibwa ofisini kwangu naomba niiandike upya ili Jumatatu niisome “ alisema Hakimu Sidoyeka. Shauri hilo lililetwa mahakamani hapo na mlalamikaji, Stephano Balthazar akimpinga Frida Swai ambaye ni mama yake mdogo kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu bibi yake aitwaye Monica Mbowe, aliyefariki mwaka 1992.Pingamizi hilo lilitolewa kwa madai ya kushindwa kukusanya, kugawa na kufunga mirathi katika kipindi cha miaka 28. Kupotea kwa karatasi za hukumu hiyo kumeibua sintofahamu katika maamuzi ya mahakama hiyo huku upande wa waleta maombi wakijawa na hofu zaidi.Hata hivyo, kumekuwa na madai kuwa nyumba moja ya marehemu iliuzwa kwa mmoja wa majaji wastaafu. Shauri hilo limeahirishwa kwa mara ya pili, ambapo Aprili 30,mwaka huu shauri hilo lilikuja mahakamani hapo kwa ajili ya kutolewa uamuzi na Hakimu Sidoyeka hakuwepo mahakamani hapo, hivyo kupangwa jana.Wasikilizaji wa pande zote mbili katika shauri hilo walifurika katika chumba cha mahakama huku kila upande ukiwa na shauku ya kutaka kujua maamuzi yatakayotolewa mahakamani hapo.Awali shauri hilo lilianza kuunguruma mahakamani hapo, Aprili 11 mwaka huu, ambapo upande wa mleta maombi, Stephano Balthazari akiwa na mashahidi sita, alimpinga msimamizi wa mirathi Frida Swai kwa madai si mwaminifu, ameshindwa kukusanya mali za marehemu na kugawa katika kipindi cha miaka 28 tangu kifo cha marehemu.Pia, alidai kuwa anao ushahidi kuwa Frida Swai amefuja mali za marehemu bibi yake kwa kuuza baadhi ya nyumba zilizoachwa ikiwemo nyumba ya Kaloleni bila kufuata taratibu. | 3 |
*Alitaka Waislamu, Wakristo wahasiwe ANAFAHAMIKA kama mungu wa kike wa Kihindu, lakini alijikuta akisakwa na polisi nchini India baada ya kwenda mafichoni kufuatia kitendo chake cha kufyatua risasi harusini. Risasi hizo zilizolenga kusherehekea tukio hilo walilokuwa wamealikwa katika hekalu la maharusi la Savitrii wilayani Karnal zilisababisha kifo cha shangazi wa bibi harusi pamoja na kujeruhi vibaya watu wengine watatu. Huyu ni Sadhvi Deva Thakur (28), kiongozi wa Wahindu wa India wa Mahasabha, ambaye alijisalimisha polisi wiki moja baada ya kwenda mafichoni. Kwenye video ya tukio hilo lililotokea Novemba mwaka jana wilayani humo, katika jimbo la Kaskazini la Haryana, Sadhvi akiwa na walinzi wake sita walionekana kwa pamoja wakifyatua risasi hewani kiholela. Mpenda bunduki huyu na watu wake ingawa ni kama walifanya kitendo hicho kama sehamu ya furaha, lakini kwa walioshuhudia walisema risasi zilirushwa hovyo mno na kuzua hofu. Ombi la ndugu na jamaa wa maharusi pamoja na meneja wa ukumbi kuwataka wasitishe ufyatuaji huo, ambao ulifanyika wakiwa jukwaani wakati wa kusakata magoma, hazikufua dafu kwani waliendeleza ujeuri na ubabe. Vyombo vya habari nchini India vinasema Sadhvi, ambalo ni jina la Kihindi linalomaanisha mwanamke aliye mtakatifu au anajiita kuwa mungu, awali alipanda jukwaani akamuomba DJ kuchezesha wimbo alioutaka. Ombi lake lilikubaliwa akaanza kucheza densi huku risasi zikifyatuliwa. Ni wakati shangazi yake bwana harusi mwenye umri wa miaka 50 Sunita Rani alipoangauka baada ya kupigwa rasasi na wengine watatu kujeruhiwa vibaya, ndipo ufyatuaji huo ambao unaelezwa kuhusisha raundi 30 ya risasi ukasitishwa. Kufuatia kitendo hicho, Makamu huyo wa Rais wa Wahindu Wote wa Mahasabha na wasaidizi wake wakatoweka mara moja eneo hilo. Polisi wakati wakiwasaka walimfungulia Sadhvi na walinzi wake sita mashitaka ya mauaji na kujeruhi. Wiki moja baadaye, Sadhvi Deva Thakur alijisalimisha mbele ya mahakama ya Karnal, akikana kuhusika na mauaji na kwamba amesikitika kuna mtu alikufa katika tukio lile. Akiwa mahakamani Thakur alisema hana hatia kwamba kuna njama dhidi yake. “Nahitaji matibabu, hii ni njama dhidi yangu, kulikuwa na watu wengine waliorusha risasi.” Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi katika Jiji la Karnal, Sadhvi aliiambia mahakama kuwa wana silaha sita wanazomiliki kihalali na kaka yake pia anayo. Polisi walikuwa wakiendelea bado na msako wa kuwasaka walinzi wake sita na walikamata magari yake mawili ya kifahari na kuliweka chini ya ulinzi hekalu lake dogo. Sadhvi Deva Thakur amekuwa mwanamke mtata mno na hivyo si mara ya kwanza kujikuta matatani. Mwaka juzi polisi walisajili kesi iliyofunguliwa kumlalamikia baada ya kutoa mwito wa kutaka Waislamu na Wakaristo wahasiwe kwa nguvu ili kuzuia idadi yao kukua. “Idadi ya Waislamu na Wakristo inakua kila siku. Kudhibiti hili, serikali inapaswa kutengeneza sheria inayozuia Waislamu na Wakristo kuzaa watoto wengi. Wanapaswa walazimishwe kuhasiwa ili wasiongezeke idadi,” aliuambia mkusanyiko wa Wahindu. Sadhvi alisema kuwa anakubaliana na baadhi ya viongozi wazalendo wa Kihindu kwamba wanawake wa Kihindu lazima wazae sana ili kukabiliana na hatari ya kugeuka dini ya wachache katika nchi yao wenyewe dhidi ya aliowaita wakuja. Deva Thakur pia alitoa kauli kuwa sanamu za miungu ya Kihindu ya kiume na kike iwekwe misikitini na makanisani. Hali kadhalika alitoa mwito sanamu ya Nathuram Godse, muuaji wa mwasisi wa India huru Mahatma Gandhi, ijengwe jimboni Haryana kwa kitendo hicho cha uuaji alichokiita cha kishujaa. Sadhvi alizaliwa na kukulia Bras, kijiji kidogo cha Wilaya Karnal, na miaka michache iliyopita alianzisha hekalu dogo kijijini hapo. Ana wafuasi wachache na wengi wao wakiwa wanakijiji wa aneo hilo. Kwa mujibu ya wanaomfahamu anafahamika kwa mitindo yake ya mavazi akiwa na umri wa miaka 27. Anaonekana kupendelea vito vya dhahabu na bunduki ambazo haishi kupozi nazo mara kwa mara. Ukurasa wake wa Facebook unaosimamiwa na kaka yake Rajeev Thakur, unamuelezea kama mkurugenzi wa Deva India Foundation na anajiita ‘mzalendo.’ Dharampal Siwach, mwanachama mwandamizi wa Hindu Mahasabha jimboni Haryana anasema alisafiri na Sadhvi kwenda makao makuu ya chama chao mjini Delhi miaka mitatu iliyopita. “Aliteuliwa kuwa makamu wa rais wa chama kitaifa baada ya mimi kuendesha kampeni kwa niaba yake,” anasema. “Lakini haikuchukua muda tukasitisha kumualika katika shughuli zetu kwa sababu alikuwa akipigwa picha akiwa na bunduki kitu kilitufehehesha.” Tukio la urushaji risasi ni ushahidi wa mapenzi yake na silaha. | 2 |
TIMU ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jana ilianza vizuri mbio zakusaka nafasi ya kucheza kwa mara ya pili mfululizo fainali za Michunao ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Afcon 2021 baada ya kuifunga Guinea ya Ikweta kwa mabao 2-1.Mchezo huo wa Kundi J ulipigwa kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, huku wageni wakiwa wa kwanza kupata bao la kuongoza lililopigwa kwa shuti kali katika dakika ya 14 na Pedro akiwa nje ya meta 18. Taifa Stars baada ya kwenda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao hil moja, lilibadilika kimchezo na kusawazisha kupitia kwa Simon Msuva aliyefanya juhudi binafsi kupata bao hilo.Msuva kwanza, alipiga mpira wa kichwa uliogonga mwamba kabla ya kuusindikiza tena wavuni kwa mguu, katika dakika ya 68 na kuibua furaha kwa mashabiki, ambao baadhi yao walianza kukata tamaa baada ya Stars kutangulia kufungwa.Taifa Stars ambayo mwaka huu ilishiriki kwa mara ya kwanza fainali za Afcom 2019 zilizofanyika nchini Misri baada ya miaka 39 iliposhiriki kwa mara ya mwisho mwaka 1980, ilipata bao lake la ushindi katika muda wa majeruhi, lililoihakikishia kuondoka na pointi zote tatu.Bao hilo lilifungwa na Salum Aboubakar katika dakika ya pili ya nyongeza (dakika ya 92), baada ya mwamuzi wa akiba kuongeza dakika nne, ambapo mfungaji alipiga shuti kali lililojaa wavuni katika nyavu ndogo na kuibua furaha kwa mashabiki waliojitokesa kuishangilia timu hiyo.Fainali hizo za Mataifa ya Afrika zitafanyika mwaka 2021 nchini Cameroon, hivyo Taifa Stars inapambana kuhakikisha inafuzu kwa mara ya pili mfululizo. Taifa Stars sasa ina kocha wa kudumu, Ettiene Ndayiragije ambaye awali alikuwa akiifundisha timu hiyo kwa muda akichukua mikoba ya Mnigeria, Emmanuel Amonike aliyetimuliwa baada ya timu hiyo kufanya vibaya katika Afcon 2019 Misri.Taifa Stars ilipoteza mechi zake zote katika fainali hizo na kumaliza ya mwisho katika hatua ya makundi. Baada ya mchezo huo, Taifa Stars sasa inakwenda Tunisia kucheza dhidi ya Libya Novemba 19 katika mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Stade Mustapha Ben Jannet. Kikosi kilichoanza Stars; Juma Kaseja, Ramdahani Kessy, Mohamed Hussein, Kelvin Yondan, Bakari Nondo, Erasto Nyoni, Salum Abubakary, Mzamiru Yassin, Simon Msuva na Farid Mussa. | 4 |
['Manchester United inafikiria kumuongezea dau kiungo wa Ureno Bruno Fernandes, 25, kabla ya Ijumaa ambayo ndiyo siku ya mwisho ya dirisha la usajili. (Guardian)', 'Ingawa Fernandes amejumuishwa katika kikosi cha Sporting kitakachominyana na Maritimo Jumanne jioni, hali inayoonesha kuwa uhamisho huo unaweza kuwa mgumu kukamilika. (Express)', 'United imeamua kumpa nafasi nyingine Alexis Sanchez mwenye umri wa miaka 31, kuonyesha uwezo wake na itamrejesha kutoka Inter Milan mwezi Juni. (Star)', 'Mashetani wekundu United hata hivyo wanaonyesha dalili ya kutotaka kufanya usajili katika dirisha hili la Januari hasa baada ya kupata mikingamo kwenye kuwanasa Fernandes na Edson Cavani wa PSG ambaye anaripotiwa kwenda klabu nyengine. (Independent)', 'Klabu ya Arsenal inatarajiwa kufanya mazungumzo na mshambuliaji wa Barcelona Pierre-Emerick Aubameyang, mwenye umri wa miaka 30. (Telegraph)', 'Arsenal imebadili vigezo walivyoweka katika mkataba wa Pablo Mari, 26 baada ya ripoti ya uchunguzi wa afya yake, na kuweka wingu jeusi juu ya uhamisho huo. (Mail)', 'Usajili wa Mari umeshindikana na beki huyo yupo njini kurudi Brazil. (ESPN)', 'Atletico Madrid inakaribia kufikia makubaliano na Cavani. (ESPN)', 'Chelsea inamfuatilia mshambuliaji wa AC Milan Krzysztof Piatek mwenye umri wa miaka 24, ambaye anawaniwa na Tottenham wakati wakijipanga kupata mbadala wa Cavani. (Telegraph)', 'Raia wa Uholanzi Steven Bergwijn, 22 amekanusha kukataa kucheza katika timu ya PSV Eindhoven siku ya Jumapili na kuwa yupo kwenye mazungumzo na Tottenham. (Sky Sports)', 'Ingawa Bergwin aliitaka PSV kumruhusu ajiunge Spurs kabla ya dirisha la usajili halijafungwa. (90min)', 'Kiungo wa Denmark Christian Eriksen, 27, anatarajiwa kuthibitishwa kuwa mchezaji wa Inter Milan siku ya Jumanne baada ya kupita vipimo vya afya usiku wa Jumatatu. (Mail)', 'Manchester United, Arsenal na Tottenham wanavutiwa kumsajili mchezaji wa Ujerumani Emre Can mwenye umri wa miaka 26 akitokea Juventus.(Metro)', 'Borussia Dortmund wanawania pia kumsainisha Can ambaye ni kiungo wa kati wa zamani wa Liverpool. (Bild - in German)', 'Mchezaji wa Tottenham Danny Rose, 29 na Kyle Walker-Peters mwennye umri wa miaka 22 wanatarajia kuondoka Spurs kwa mkopo kabla ya siku ya mwisho ya usajili. (Standard)', 'Saints wamejipanga kumsajili Walker-Peters kwa mkopo, huku wakiendelea na majadiliano kuhusu mkataba wake kama utajumuisha malipo ya paundi milioni 12 kuwa sehemu ya mkataba wake . (Mail)', 'Aston Villa imewasilisha dau la usajili la pauni milioni 4.2 kwa mchezaji wa zamani wa Chelsea na Liverpool, Daniel Sturridge, 30 kutoka klabu ya Uturuki ya Trabzonspor. (Talksport)', 'West Ham wanajipanga kumsajili mchezaji wa Tottenham na Argentina Juan Foyth, 22. ', 'Klabu hiyo pia iko kwenye mazungumzo na Slavia Prague juu ya kiungo wa kiungo Tomas Soucek, 24. (Guardian)'] | 4 |
VINARA wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Yanga leo wanashuka dimbani kwenye Uwanja wa CCM, Kambarage Shinyanga kusaka pointi tatu katika mchezo dhidi ya Stand United. Yanga na Stand United mara ya mwisho kukutana ilikuwa raundi ya kwanza zilipofungana mabao 4-3 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa.Kipa Klaus Kindoki hatosahau mchezo huo uliompa presha kubwa akionekana kushindwa kumudu hali iliyosababisha baadhi ya mashabiki kumponda kwa kufungwa mabao kizembe. Kwa mara nyingine anakutana nao huenda akawa makini zaidi awamu hii kwani tayari amepata uzoefu baada ya kufanya vizuri katika mechi zilizopita. Yanga pia, haitamsahau mshambuliaji wa Stand Alex Kitenge aliyewafunga ‘Hat trick’ katika mchezo wa raundi ya kwanza.Bila shaka mchezaji huyo anahitaji kuchungwa. Stand United licha ya kuwa ina wachezaji wengi wazuri wa ndani na nje ya nchi, haiko katika mwenendo mzuri. Katika michezo 21, imeshinda sita, sare tatu na kupoteza 12 ikishika nafasi ya 17 kwa pointi 21.Ikipoteza mchezo wa leo basi itazidi kujiweka kwenye hatari ya kushuka daraja hivyo, inahitaji kupambana kujiondoa ilipo. Inakutana na Yanga iliyoko vizuri kileleni kwa pointi 53 ikiwa na rekodi ya kutopoteza mchezo wowote katika michezo 19, ikishinda 17 na kupata sare mbili. Timu hiyo ya Jangwani imekuwa ikifanya vizuri kwenye uwanja wa nyumbani na hata ugenini.Je, itaendeleza rekodi hiyo au itavunjwa? Mechi nyingine itakayochezwa leo ni Azam FC dhidi ya Mwadui, ikitarajiwa kuwa na kisasi baada ya ule uliopita wa raundi ya kwanza kutoka sare ya bao 1-1 ugenini mkoani Shinyanga.Azam FC imeshindwa kufanya vizuri katika mchezo uliopita wa ligi dhidi ya Ruvu Shooting ikitoka kupata sare ya bila kufungana 0-0 na kuzidi kuipa Yanga nafasi ya kubaki kileleni kwa pointi nyingi.Timu hiyo inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi 41, tofauti ya pointi 12 dhidi ya Yanga inayoongoza. Imeshacheza michezo 18, imeshinda 12, sare tano na kupoteza mmoja.Mchezo wa leo ni muhimu kwao kushinda kuendelea kuwa katika mbio za ubingwa wa ligi. Mwadui inashika nafasi ya 11 ikiwa na pointi 24, imecheza michezo 22, imeshinda sita, sare sita na kupoteza 10. Ikipoteza itakuwa kwenye nafasi ya kushuka zaidi chini hivyo, inahitaji ushindi ili kupanda katika nafasi za juu | 4 |
Na JUSTIN DAMIAN,
SEHEMU nyingi duniani, watu wanapenda kunywa kahawa ingawa kwa hapa Tanzania wanywaji ni wachache. Kahawa husaidia kumfanya mnywaji kujisikia vizuri baada ya muda mwingi wa kufanya kazi. Hata hivyo, wapo baadhi ya watu ambao hufikiri kuwa kahawa ni mbaya kwa afya.
Lakini utafiti mpya uliofanywa na Chuo Kikuu cha Edinburg na Southmpton nchini Uingereza umeonyesha kuwa unywaji kahawa unamlinda mnywaji kupata ugonjwa wa saratani ya ini ambao ni hatari na hauna tiba.
Watu ambao wanaiponda kahawa wanasema, kinywaji hicho kina caffeine ambayo inasababisha ugonjwa wa moyo na kuwafanya wanaougua magonjwa ya moyo kufariki mapema zaidi. Tofauti na mtizamo huo, sasa wanasayansi wanasema utumiaji mzuri wa kahawa unaweza kumwepusha mtumiaji na hepatocellular carcinoma ambayo ni aina ya saratani ya ini.
Timu kubwa ya watafiti walichunguza data kutoka kwenye tafiti 26 zilizohusisha zaidi ya washiriki milioni mbili. Watafiti hao waliobobea kwenye masuala ya afya ya umma, waligundua kuwa saratani ya ini aina ya hepatocellular carcinoma ilikuwa ikiwaathiri takribani watu 50 katika kila watu 1000 waliwachunguza katika utafiti huo. Hata hivyo, waligundua kuwa katika kundi la wanywaji wa kahawa, watu 33 walionekana kuwa wameathirika kati ya watu 1000 ikiwa ni upungufu wa asilimia 40 ukilinganisha na kundi la wasiokunywa kahawa.
Watafiti hao pia waligundua kadiri unavyokunywa kahawa zaidi, ndivyo ambavyo unapunguza uwezekano wa kupata aina hii ya saratani. Timu hiyo ilisisitiza kuwa unywaji wa kikombe kimoja cha kahawa yenye caffeine inapunguza uwezakano wa kupata ugonjwa huo usio na tiba kwa asilimia 20 huku unywaji wa vikombe viwili vya kahawa ukiwa unapunguza uwezekano kwa asilimia 35.
Hepatocellular carcinoma inashika nafasi ya pili kati ya magonjwa wa saratani yanayoongoza kwa kusababisha vifo duniani. Kujilinda dhidi ya ugonjwa huu ni jambo jema kwa kuwa hauna tiba lakini pia wanasayansi hao wanasisitiza unywaji kahawa uliopindukia si salama kwa afya ya mtumiaji na hivyo kuwataka watumiaji watumie kwa kiasi.
Wanasayansi wanawezaje kujua ni kiasi cha kahawa mnywaji akitumia hakiwezi kumletea madhara ya kiafya? Dk. Oliver Kennedy wa Chuo Kikuu cha Southampton anasema; “hatua inayofuata ni kwa watafiti kuchunguza ufanisi kupitia utafiti usiochagua sampuli maalum kwa kuzingatia wanywaji wa kahawa ambao wapo katika hatari ya kupata ugonjwa huu, watu wengi walichangia katika mafanikio ya utafiti huu.”
Pamoja na faida hiyo, unywaji kahawa una faida nyingi ikiwamo kupunguza maumivu ya misuli baada ya kazi. Unywaji kahawa wa kiasi pia unapunguza uwezekano wa kupata ungonjwa kisukari namba mbili – Diabetes Type 2. Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Havard nchini Marekani unaonyesha kuwa unywaji wa kikombe kimoja cha kahawa kwa siku unapunguza uwezekano wa kupata aina hiyo ya kisukari kwa asilimia tisa.
Unywaji kahawa pia unapunguza uwezekano wa kujiua pamoja na mfadhaiko (depression). Utafiti uliofanyika kwa kipindi cha maika 10 uliohusisha wauguzi wanawake 86,000 ulionyesha kupungua kwa uwezekano wa kujiua kwa wale waliokuwa wakitumia kahawa. Utafiti mwingine ulifanyika na Shule ya Afya ya Umma ya Chuo Kikuu cha Havard nchini Marekani ulionyesha kuwa wanawake wanaokunywa vikombe vine au zaidi vya kahawa wanapunguza uwezekana wa kupata mfadhaiko kwa asilimia 20. | 0 |
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM KATIBU Mkuu wa Klabu ya Simba, Patrick Kahemele, amesema ubingwa walioupata juzi katika mashindano ya ligi ya vijana chini ya miaka 20, umewafungulia njia ya kufanya vizuri kwenye michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu. Kikosi cha Simba B kilifanikiwa kunyakua ubingwa baada ya kuifunga Azam FC kwa jumla ya penalti 5-3, katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kwa dakika 120 zilizomalizika kwa sare ya mabao 2-2. Baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Kahemele aliliambia MTANZANIA kuwa, kikosi cha timu ya vijana kimekuwa kikitoa wachezaji wazuri ambao majina yao hupata sifa kubwa kwa baadaye. “Huu ni mwanzo tu, kwani msimu huu tumejipanga vizuri ili kuhakikisha timu yetu kubwa inatwaa ubingwa wa ligi kuu, Kombe la FA na Kombe la Mapinduzi,” alisema. Wakati huo huo, Kocha Mkuu wa timu ya Azam, Iddy Nassor, alisema wachezaji wake walijitahidi kucheza soka safi hadi kufanikiwa kuingia hatua ya fainali, ingawa walishindwa kutwaa ubingwa. “Pamoja na wachezaji wetu kucheza kwa muda mrefu bila kupata muda wa kupumzika, lakini walijitahidi kupambana kuwania kutwaa ubingwa, ingawa bahati haikuwa upande wetu. “Hata hivyo, tuliwakosa wachezaji wetu muhimu ambao walikuwa kwenye timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys, kutokana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuzuia kadi zao,” alisema. | 4 |
['Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Arsenal inamtaka nahodha wa zamani wa klabu hiyo Mikel Arteta kuchukua mikoba ya kocha aliyetimuliwa Unai Emery. Kwa sasa Arteta ni kocha msaidizi wa Pep Guardiola katika klabu ya Manchester City. (Mirror)', 'Arsenal ipo tayari, ikibidi, kupitia rekodi na kufanyia usaili mpaka wakufunzi 12 ambao watawania nafasi iliyoachwa wazi na Emery aliyetimuliwa juma lililopita. (Mirror)', 'Hata hivyo, klabu hiyo inaweza kumpa mkataba wa kudumu kocha wao wa muda kwa sasa Freddie Ljungberg, 42, endapo atafanya mapinduzi makubwa ya matokeo ya michezo yao. (Evening Standard)', 'Everton wanatarajiwa kutomfukuza kocha wao Marco Silva kabla ya mchezo na mahasimu wao wa jadi Liverpool hapo kesho Jumatano. (Express)', 'Kocha Manuel Pellegrini amejiongezea muda wa kuifunza klabu ya West Ham baada ya kuifunga Chelsea. Kibarua cha kocha huyo mzoefu pia kipo mashakani kutokana na timu yake kutokuwa na matokeo mazuri. (Mail)', 'Katika harakati za kuimarisha kikosi, West Ham wanataraji kusajili golikipa, kiungo na mshambuliaji katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari. (Star)', 'Kocha aliyetimuliwa na klabu ya Tottenham hivi karibuni Mauricio Pochettino amefungua milango ya kurejea katika ligi ya Primia akitamba kuwa yupo tayari kuzamia tena kwenye bahari ya ukufunzi. (Fox Sports, via Mirror)', 'Mlinzi wa Tottenham Jan Vertonghen, 32, anaamini Pochettino amekuwa mhanga wa mafanikio yake mwenyewe klabuni hapo na kuwa wachezaji wote wanahisi kusababisha kufutwa kazi kwa kocha huyo raia wa Argentina. (Evening Standard)', 'Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uswidi Zlatan Ibrahimovic, 38, anatarajiwa kugoma kurejea katika ligi ya Primia na badala yake kusaini mkataba na klabu yake nyengine ya zamani ya AC Milan. (Telegraph)', 'AC Milan pia wamepewa ofay a kumsajili mshambuliaji wa Chelsea na Ufaransa Olivier Giroud, 33. (Calciomercato)', 'Kiungo mshambuliaji wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen, 27, ameweka wazi msimamo wake kuwa hatoingia makubaliano mapya na klabu yake ya sasa na atakataa ushawishi wowote ule utakaolenga kumbakiza Spurs. (Telegraph)', 'Kocha wa Crystal Palace Roy Hodgson amesema anatumai kuendelea kusalia na mshambuliaji raia wa ays Ivory Coast Wilfried Zaha, 27, katika klabu hiyo mpaka mwisho wa mkataba wake mwaka 2023. (Sky Sports)', 'Real Madrid wanajiandaa kutuma ofay a usajili kwa beki wa Napoli na timu ya taifa ya Senegali Kalidou Koulibaly, 28, ambaye amekuwa akiwidwa kwa muda sasa na Manchester United. (Calciomercato)', 'Klabu ya AS Roma wanajipanga kutunisha ofa ya kumsajili moja kwa moja mlinzi wa Manchester United Chris Smalling, 30. Mchezaji huyo kwa sasa yupo kwa mkopo na Roma. (Il Romanista, via Manchester Evening News)'] | 4 |
Benjamin Masese, Mwanza Jeshi la Polisi mkoani Mwanza
limesema hakuna viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wala
wasaidizi wa Katibu Mkuu wa chama hicho. John Mnyika waliotekwa mkoani humo isipokuwa
walishikiliwa kwa mahojiano. Amesema hatua hiyo ilikuja baada
ya wananchi wa Kata ya Mahina kutoa taarifa kwamba si watu wema. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Desemba 30, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro amesema taarifa zilizosambaa tangu juzi katika mitandao ya kijamii kwamba wanachama wa Chadema ambao ni wasaidizi wa Mnyika wametekwa si za kweli na kuwataka wananchi kuzipuuza. “Viongozi waliokuwa wameshikiliwa
na polisi ni Katibu wa Katibu Mkuu wa Chadema, Abdulkarim Muro (31) na dereva
wa Mnyika, Said Haidani (30) na walikuwa mikononi kwa polisi tangu juzi saa 12
jioni baada ya raia wema kutoa taarifa polisi kwamba kuna watu wawili wanahisiwa
si wema na wamekuwa wanaingia katika nyumba moja iliyopo karibu na Hoteli ya
Paradise. “Baada ya taarifa hizo polisi walifuatilia kwa haraka na kufanikiwa kuwakamata na walipotakiwa kutoa maelezo ya awali ya utambulisho waligoma na kulazimika kuwapeleka katika kituo kikuu cha kati, hivyo baada ya polisi kujiridhisha tumewachia na wanaendelea na shughuli zao,” amesema Muliro. | 3 |
Na Mwandishi Wetu – Dodoma
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema amebaini kuwa kero nyingi za wananchi hazitatuliwi na viongozi wa ngazi ya chini kwa sababu mikutano ya vijiji, kata na mitaa imekuwa haifanyiki kama inavyotakiwa kisheria.
Kauli hiyo aliitoa mjini hapa bungeni juzi wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa sita wa Bunge la 11.
“Azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kumtumikia kila Mtanzania popote pale alipo. Lakini nimebaini baadhi ya kero za wananchi ambazo zingeweza kutatuliwa katika ngazi za wilaya, zinaletwa kwenye ofisi za viongozi wa kitaifa, au zinasubiri ziara za viongozi hao.
“Nawasihi viongozi wa mikoa na halmashauri tembeleeni vijijini na mtatue kero za wananchi huko vijijini, pia hakikisheni mikutano ya vijiji iliyowekwa kwa mujibu wa sheria inafanyika na maazimio yake yanafika katika vikao halali vya uamuzi. Wabunge, ninyi ni sehemu ya halmashauri zenu, nawasihi toeni msukumo unaostahili,” alisema.
Pia alisema suala la kutotatua kero za wananchi katika ngazi ya Serikali za Mitaa ni kinyume na dhamira ya Serikali ya kuwatumikia wananchi wote bila ubaguzi, ambalo pia ni kinyume na msimamo wa Ibara ya 146 (1) ya Katiba ya Tanzania.
Akinukuu ibara hiyo alisema: “Madhumuni ya kuwapo Serikali za Mitaa ni kupeleka madaraka kwa wananchi. Na vyombo vya Serikali za Mitaa vitakuwa na haki na mamlaka ya kushiriki na kuwashirikisha wananchi katika mpango wa shughuli za utekelezaji wa maendeleo katika Serikali zao na nchi kwa ujumla.”
Akisisitiza suala hilo, alisema Sheria ya Serikali za Mitaa inaelekeza kuitishwa kwa mikutano mikuu ya vijiji kila baada ya miezi mitatu, pia inatoa fursa ya kuitishwa kwa mikutano ya dharura endapo ipo haja ya kufanya hivyo.
“Kutokana na msimamo huo wa kisheria na kutokana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kutatua kero za wananchi, suala la utatuzi wa kero za wananchi halitakiwi kuendelea kusubiri ziara za viongozi, badala yake, kero hizo zitatuliwe katika ngazi zinazohusika na zitatuliwe kwa wakati,” alisisitiza.
Alisema watendaji wa kata, vijiji na mitaa hawana budi kuitisha mikutano ya kisheria ya vijiji, kata na mitaa na kusoma taarifa za mapato na matumizi ya miradi ya maendeleo katika maeneo yao.
Aliwataka viongozi na watendaji katika ngazi ya mkoa, wilaya na halmashauri wajenge utamaduni wa kuwatembelea wananchi vijijini na kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili, ikiwa ni pamoja na kuzitafutia ufumbuzi. | 3 |
Meneja wa wachezaji hao Jamal Kasongo alisema jana kuwa wachezaji hao walijaribiwa katika baadhi ya michezo ya kirafiki iliyochezwa huko na kuonekana kufanya vizuri.Wachezaji hao walikwenda TP Mazembe kwa majaribio ya siku 10 ambapo Kasongo alisema yeye kama Meneja alielezwa kuwa wamefanya vizuri na timu hiyo imepeleka mazungumzo mezani katika timu ya Stand United.“TP Mazembe alinipa taarifa kuwa wachezaji wamefanya vizuri na kutokana na utaratibu wao wanakwenda wenyewe kuzungumza na Stand United kwa hiyo wakikubaliana watatangaza rasmi kama wanawachukua,”alisema.Iwapo watafanikiwa kusajiliwa na timu hiyo ya Congo, wataungana na wachezaji wengine wa Tanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao wanachezea kwa muda mrefu.Samatta na Ulimwengu bado wanaendelea kupambana na kuhakikisha wanaondoka katika timu hiyo msimu huu na kwenda kucheza soka Ulaya.Wakati Samatta akitarajiwa kwenda Ubelgiji katika timu ya Genk, Ulimwengu anataka kwenda St. Ettiene ya Ufaransa.Kuondoka kwao katika timu hiyo kutatoa fursa kwa wachezaji hao kupata nafasi hiyo baada ya kuonesha kiwango kinachotakiwa. | 4 |
MACHAKOS, KENYA Muigizaji maarufu nchini Kenya, Jamal Nasoor maarufu (Baba Junior) aliyejipatia umaarufu kupitia mchezo wa kuigiza runingani wa Vioja Mahakamani akicheza kama Hakimu, ameuwawa na mpenzi wake anayetambulika kwa jina la Grace Kanamu. Kifo cha Jamal ambaye ametamba pia katika tamthilia ya Junior iliyokuwa ikionyeshwa kupitia Televisheni ya KTN, kinaripotiwa kutokea Jumanne Desemba 11 baada ya kutokea majibishano kati yake na mpenzi wake huyo waliopokuwa katika sherehe iliyofanyika katika klabu moja ya usiku hoteli ya Arks. Imeelezwa kuwa baada ya majibishano hayo Grace alichukua kisu na kumchoma Jamal na kusababisha kifo chake. Baada ya kuchomwa kisu Jamal alikimbizwa katika hospitali ya Shalom lakini jana Desemba 12 arifariki dunia, Polisi wamesema bado wanaendelea na uchunguzi wa kifo hicho. Aidha inasemekana Jamal na Grace walikuwa majirani katika eneo walilokuwa wanaishi la Syokimau katika kaunti ya Machakos na walianza kuwa na uhusiano uliodumu kwa miezi Tisa baada ya wote wawili kutalikiana na wenza wao. | 2 |
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeahidi kuandaa Ilani bora ya Uchaguzi 2020-2025, itakayotoa kipaumbele na kuwanusuru wakulima, hasa wadogo na watanzania wote kutoka katika lindi la umasikini.Akizungumza na waandishi wa habari juzi mjini Iringa, Mwenyekiti wa Chadema wa Kanda ya Nyasa inayojumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe na Rukwa, Mchungaji Peter Msigwa alisema chama chao kinakusudia kufanya mageuzi makubwa ya kilimo, endapo kitachaguliwa kuongoza serikali.“Tunakusudia kuongoza serikali itakayofanya mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo kwa kuchochea na kufungua fursa kubwa za masoko ya ndani na nje ya nchi ya mazao ya kilimo na mifugo,” alisema.Mchungaji Msigwa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, alisema kwa kupitia Ilani hiyo wanakusudia kuongoza serikali (endapo watachaguliwa), itakayoimarisha taasisi za kifedha na kuzijengea mazingira mazuri ya kuelekeza uwekezaji wa fedha kwenye kilimo.“Tutatengeneza mazingira mazuri sawa na ambavyo mikopo na mitaji mikubwa imekuwa ikielekezwa kwenye biashara na sekta nyingine ili sekta hii ya kilimo iliyoajiri watanzania wengi iwe na tija,” alisema.Alisema Chadema inakusudia kurasimisha mashamba na mali za wakulima ili kuwawezesha wakulima wakubwa na wadogo, waweze kukopesheka na kupata mitaji kwa haraka na kwa urahisi ili waweze kutanua wigo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.Mchungaji Msigwa alisema serikali yao itatenga na kuidhinisha bajeti kubwa kwa ajili ya kugharamia sekta ya kilimo, kwa kutenga fedha nyingi kwa ajili ya mbolea na pembejeo zote za kilimo ili zimfikie mkulima kwa wakati na kwa unafuu mkubwa. Kuhusu vyama vya ushirika na umuhimu wake kwa sekta hiyo, Msigwa alisema wataimarisha vyama vya ushirika vilivyokufa kwa kuviwezesha kuwa msaada wa kweli kwa wakulima wa kawaida.“Lakini pia tutaimarisha viwanda vngi vya kuchakata mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi vijijini ili kuongeza thamani ya mazao hayo na hatimaye kumuongezea mkulima kipato kitakachomkwamua kutoka kwenye umasikini,” alisema.Akizungumzia miundombinu ya barabara zinazolalamikiwa na wakulima kuwa kero katika shughuli zao za kilimo na biashara ya mazao yao, alisema watajenga na kuboresha miundombinu ya barabara za vijijini.Alisema hatua hiyo itawawezesha wakulima kupata pembejeo kwa urahisi na kusafirisha mazao yao moja kwa moja kutoka vijijini mwao hadi kwenye masoko ya mazao yaliyopo katika miji mikubwa nchini. Msigwa alizitaja sekta zingine zitakazopewa kipaumbele na chama chao kuwa ni afya, maji na elimu. | 3 |
Na JANETH MUSHI-ARUSHA UAMUZI wa kuongezewa muda wa kuwasilisha notisi ya nia ya kukata rufaa dhidi ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, unatarajiwa kutolewa Desemba 20, mwaka huu na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha. Uamuzi huo utatolewa baada ya Lema jana kufanikiwa kuwasilisha maombi yake ya kuongezewa muda wa kuleta notisi hiyo ya rufaa dhidi ya dhamana yake baada ya mahakama hiyo kutupilia mbali pingamizi mbili za mawakili wa Serikali waliokuwa wakitaka maombi hayo yasisikilizwe. Mbele ya Jaji Dk. Modesta Opiyo wa mahakama hiyo, upande wa Jamhuri ulikuwa ukiwakilishwa na Wakili Hashim Ngole, Matenus Marandu, Elizabeth Swai na Adelaide Kasala huku Lema akitetewa na Wakili Sheck Mfinanga na Faraji Mangula. Katika maombi hayo namba 69 ya mwaka huu, baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, Jaji Dk. Opiyo alisema kuwa atatoa uamuzi huo siku hiyo saa sita mchana. “Baada ya kusikiliza hoja za pande zote nitatoa uamuzi Jumanne ijayo saa sita mchana, msije asubuhi ili nipate muda wa kupitia hoja zenu,” alisema Jaji Dk. Opiyo. Awali, akitoa uamuzi wa pingamizi mbili zilizotolewa Desemba 14, mwaka huu na mawakili hao wa Jamhuri, Jaji Dk. Opiyo, aliyesoma uamuzi huo kwa muda wa dakika 50 kuanzia saa 5:30 asubuhi hadi saa 6:20 mchana, alisema ameamua kuzitupa pingamizi hizo baada ya kuziona hazina mashiko ya kisheria. Alisema kuwa hakuna maombi kama hayo yaliyoacha kusikilizwa mahakamani kwa kushindwa kuonyesha kifungu namba 392 A cha sheria ya uendeshaji wa mashauri ya jinai hivyo akalitupa pingamizi la kwanza la mawakili wa Serikali waliodai maombi hayo hayakufuata utaratibu wa kisheria ikiwemo kutoonyesha vifungu vya sheria waliyoitumia kuleta maombi hayo. “Baada ya kupitia hoja za pande zote, mahakama imeamua kutupa pingamizi hizo za Jamhuri baada ya kuziona kuwa hazina mashiko kisheria na hata upande wa Jamhuri ulishindwa kurejea shauri lolote ambalo limewahi kufanyiwa uamuzi na mahakama za juu kuhusu suala hilo,” alisema Jaji Dk. Opiyo. Akizungumzia hoja ya pili ambayo Jamhuri ilidai ya kiapo kinachounga mkono maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo kimekosewa hivyo hakifai kwa sababu wamejumuisha mambo yasiyotakiwa kisheria ikiwemo maoni, mabishano na hitimisho na kubeba hoja za rufaa alisema mahakama hiyo imeondoa aya ya 11 na 12. Alisema kuwa aya nyingine za 9, 10, 13 na ile ya 17 zitabaki katika hati hiyo ya kiapo kwa sababu hazibebi hoja za rufaa, maoni, mabishano wala hitimisho hivyo mahakama hiyo haiwezi kukataa hati hiyo ya kiapo iliyoambatanishwa na maombi hayo. MAOMBI YA KUONGEZEWA MUDA Akiwasilisha hoja za maombi ya kuongezewa muda wa kuwasilisha notisi hiyo ili rufaa hiyo iweze kusikilizwa, Wakili Mfinanga, alidai mahakamani hapo kuwa maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo chini ya kifungu 361(2) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai. Alidai kuwa uamuzi wanaotarajia kukatia rufaa ni uliotolewa Novemba 11, mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na Hakimu Desderi Kamugisha, ambapo Lema anakabiliwa na kesi namba 440 na 441 za uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli. Alitaja sababu mbili za msingi za kukatia uamuzi huo rufaa kuwa ni kuiomba mahakama hiyo ipitie makosa ya kisheria yaliyofanywa na mahakama ya chini na kusema kuwa uamuzi huo ulimpa mleta maombi (Lema) dhamana ila kabla hajapewa masharti ya dhamana upande wa Jamhuri ulitoa notisi ya nia ya kukata rufaa. “Kwa msingi huo mahakama ilisema imefungwa mkono na hawawezi kuendelea na jambo lolote kuhusu suala hilo hata uamuzi wake wa kumpa dhamana haukuwezwa kutimizwa na mahakama haikueleza upande wowote ambao haujaridhika na uamuzi huo una haki ya kukata rufaa,” alidai Mfinanga na kuongeza: “Kuna vitu muhimu na vitasahihishwa iwapo tutaleta notisi ya nia ya kukata rufaa na rufaa yenyewe kusikilizwa na mahakama yako ambayo ni msimamizi wa haki na sheria ikatoa ruksa ili tuweze kusikilizwa na rekodi ya mahakama ya chini iweze kurekebishwa, ni muhimu mahakama kuzingatia maombi haya pasipo kuzingatia mambo mengine.” Huku akirejea mashauri mbalimbali ya mahakama za juu, aliendelea kueleza mahakama hiyo kuwa mahakama ikishasema imempa mtu haki ya dhamana lazima itaje masharti ya dhamana. “Tunaomba mahakama itupatie muda tena mfupi ambao hautazidi hata saa 1:30 kwa ajili ya kuleta notisi hiyo ili mahakama iweze kurekebisha makosa hayo,” alisema. Akiwasilisha hoja ya pili, Wakili Mangula, alidai mahakamani hapo kuwa tangu kutolewa kwa uamuzi huo hawajapumzika na muda wote walikuwa mahakamani. Alidai kuwa walikuwa wanaenda mahakamani kwa njia tofauti ili kuiomba mahakama irekebishe makosa hayo ya kisheria. Alidai kuwa baada ya uamuzi huo kutolewa muda wa kazi ulishaisha na ilikuwa Ijumaa hivyo Novemba 14, mwaka huu walipeleka barua ya malalamiko mahakamani hapo na walipoitwa pande zote mbili katika shauri namba 6 lakini walikumbana na pingamizi zilizowasilishwa na mawakili wa Serikali. “Novemba 22, mahakama ilitoa uamuzi na kututaka waleta maombi tukate rufaa na hapo mleta maombi alipata haki yake ya kukata rufaa ambayo haikuelezwa mahakama ya chini na tulitoa notisi tukiamini tuko ndani ya muda na hatimaye rufaa ililetwa mbele ya Jaji Mfawidhi Fatuma Masengi,” alidai. Alieleza mahakama hiyo kuwa katika rufaa hiyo namba 113, walikutana tena na pingamizi la Serikali kuwa wametoa notisi ya rufaa hiyo nje ya muda wa siku moja hivyo hizo ni jitihada walizokuwa wakifanya na si wazembe, wajinga wa sheria kama ilivyodaiwa na wakili wa Serikali. Akijibu hoja za waleta maombi hao, Wakili Ngole, alidai kuwa ni wazembe, wajinga wa sheria na kuwa hata uamuzi wanaolalamikia mahakamani hapo ambao awali ulimpa mleta maombi dhamana, lakini kabla hajapewa masharti ya dhamana mahakama iliingiliwa mamlaka yake hawajawasilisha na maombi hayo. Wakili huyo alidai mahakamani hapo kuwa hakukuwa na makosa yoyote ya kisheria kama inavyodaiwa na waleta maombi hao na kudai kuwa baada ya hakimu kusema mahakama inampa mshtakiwa dhamana Jamhuri kwa haki yake walisimama na kuifahamisha mahakama wana nia ya kukata rufaa. “Ni utaratibu wa kisheria kuwa panapokuwa na notisi ya nia ya kukata rufaa mahakama haiwezi kuendelea na jambo lolote kuhusiana na kesi hiyo, hivyo hakimu asingeweza kuendelea na kesi na inafahamika notisi inasimama badala ya rufaa,” alidai na kuongeza: “Kwa mujibu wa kifungu 359(1) na 361(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, vinaeleza mtu ambaye hajaridhika na hatua yoyote au uamuzi uliotolewa au kupitishwa anaweza kukata rufaa mahakama za juu.” Lema anashikiliwa kwa zaidi ya mwezi mmoja katika mahabusu ya Gereza Kuu la Kisongo baada ya kukamatwa Novemba 2, mwaka huu nje ya Viwanja vya Bunge mjini Dodoma ambapo alifikishwa mahakamani Novemba 8, mwaka huu akikabiliwa na mashtaka ya uchochezi dhidi ya Rais Dk. Magufuli. | 3 |
GYM ya kisasa nchini ya Bodystreet imempatia ofa ya masomo nchini Ujerumani mchezaji bora wa mashindano ya Kombe la Cosafa 2019 kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 iliyomalizika wiki iliyopita nchini Afrika Kusini.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu na mwanzilishi wa Bodystreet hapa nchini, Emma Lehner Lyayuka amesema wameamua kumpatia Enekia Kasonga ofa ya masomo nchini Ujerumani, baada ya kuridhika na kipaji chake.Pia mbali na kusoma masomo hayo ya michezo, pia atakuwa akicheza soka katika timu ya wanawake ya FFC Wacker München ya Munich, Ujerumani katika kipindi chote atakachokuwa akisoma.Kasonga ambaye anaichezea Alliance Queens ya Mwanza, alikuwa mchezaji bora katika mchezo wa Tanzania (Tanzanite) dhidi ya Afrika Kusini, ambapo Tanzania ilishinda 2-0 na yeye alifunga bao moja.Pia alifunga jumla ya mabao manne katika mashindano hayo. Pia mchezaji huyo alifunga bao pekee la Tanzania wakati ilipofungwa 2-1 na Zambia katika hatua ya makundi na kuifanya kumaliza ya pili na kutinga nusu fainali.Lyayuka alisema kuwa walimuona Enekia katika mchezo wa Tanzanite na Afrika Kusini wa Kombe la Cosafa na walivutiwa sana jinsi alivyokuwa akicheza na kuisaidia Tanzania kutwaa ubingwa wa mashindano hayo kwa mwaka huu.Alisema wanafanya mawasiliano na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili kukamilisha taratibu mbalimbali za kumwezesha mchezaji huyo kwenda kusoma Ujerumani mafunzo ya kuanzia miezi mitatu hadi mwaka.Wakati wa kutangaza ofa hiyo, Bodystreet waliwaonesha waandishi wa habari vifaa vya teknolojia ya kisasa vya kufanyia mazoezi, ambavyo ni vya kwanza kuwepo nchini.Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi alifanyishwa mazoezi kupitia vifaa hivyo, ambapo alikiri kuwa vinabana muda na mtu anafanyishwa mazoezi katika viungo vyote.Bayi alisema kuwa gym hiyo inasaidia sana kubana muda kwani mtu hatumii muda mwingi, lakini mwili mzima unafanyishwa mazoezi kutokana na kizibao anachokivaa wakati wa mazoezi.Juhudi za kuwapata viongozi wa Alliance na TFF ili kuzungumzia ofa hiyo jana hazikufanikiwa baada ya baadhi yao simu zao kutopatikana kabisa na wengine ziliita bila majibu. | 4 |
TAASISI ya Teknolojia ya Dar es Dar es Salaam (DIT) imeendesha mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa walimu 540 wa shule mbalimbali za serikali nchini.Taarifa iliyotolewa na DIT inaeleza kuwa mafunzo hayo ya siku tano (Oktoba 21- 25, 2019) yalikuwa na lengo la kuwapa uwezo watumishi hao wa utunzaji wa vifaa vya TEHAMA ambavyo hutolewa kwa shule mbalinbali nchini na serikali pamoja na wadau wengine.vifaa hivyo ni pamoja na kompyuta, printa na vifaa vingine vya mawasiliano.Mafunzo hayo yaliyotolewa na wataalamu wa DIT yamefadhiliwa na Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (UCSAF) ambapo walimu waliopata fursa hiyo wanatoka katika shule za msingi na sekondari kutoka mikoa kadhaa nchini.“Walimu tuliowapokea hapa ni 540 na mafunzo haya yanaanza leo Jumatatu na yanafungwa Ijumaa, ni mafunzo ya siku tano,” alisema Mratibu wa Mafunzo kutoka DIT, Daudi Mboma.Walimu hao ni kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Iringa, Pwani, Mtwara, Ruvuma, Lindi, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Dodoma, Zanzibar na Tanga. | 3 |
Na FERDINDA MBAMILA-DAR ES SALAAM WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa na Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini, Inmi Patterson, wamezindua kampeni ya maadhimisho ya miaka 15 ya ubia kati ya Marekani na Tanzania katika kupambana na janga la VVU/Ukimwi, chini ya Mpango wa Rais wa Marekani wa Kupambana na Ukimwi (PEPFAR). Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana, ambako Kaimu Balozi alitangaza pia kuwa, hivi karibuni PEPFAR imevuka lengo muhimu katika utoaji huduma hapa nchini, ambako hivi sasa inatoa matibabu yanayookoa maisha kwa zaidi ya Watanzania milioni moja wanaoishi na VVU. Alisema tangu kuzinduliwa kwa PEPFAR na Rais George W. Bush hapo mwaka 2003, Serikali ya Marekani imewekeza zaidi ya Dola za Kimarekani bilioni 4.5 (takriban Sh trilioni 10.26) katika kudhibiti maambukizi ya VVU/Ukimwi nchini. “Kampeni mpya ya PEPFAR15 itaendelea kwa mwaka huu ili kuadhimisha mafanikio yaliyofikiwa na nchi zetu mbili katika mapambano dhidi ya VVU na kuendelea kuchukua hatua stahili za kudhibiti kuenea kwa VVU nchini Tanzania. “Wakati wa kampeni hii, tutafanya kazi nanyi nyote, pamoja na watu wanaoishi na VVU nchini kote Tanzania, ili kusimulia hadithi na habari nzuri (positive stories); habari za watu wanaoishi na VVU ambao wakati mmoja walikuwa dhaifu na wagonjwa. “Lakini sasa wakiwa wenye nguvu na afya, habari za watu waliopima mapema na kuanza matibabu hata kabla hawajaanza kuumwa, habari za watu wanaoishi na VVU walioanza matibabu ya kuokoa maisha ili pia kuwalinda wenza wao na habari za akina mama wanaoishi na VVU wanaopata matibabu ili kuwalinda watoto wao,” alisema Kaimu Balozi Inmi Patterson. | 2 |
Mwadui imekuwa ya kwanza kuitibulia Simba kwa kupata sare hiyo baada ya wekundu hao wa Msimbazi kushinda mfululizo takriban mechi tano. Mabao yote hayo Simba ndio ilianza kufunga kabla Mwadui haijachomoa.Mwadui walionekana kucheza mpira wa kasi na kujituma muda wote huku ikionekana kuhitaji kupata matokeo ya ushindi kiasi kilisababisha Simba kupotea eneo la kati pamoja na kupoteza mipira mara kwa mara.Nahodha huyo alisema kipindi cha kwanza walikuwa wakiwasoma Simba ili wafahamu sehemu muhimu za kuwakamata vinara hao kisha waanze kupambana, ingawa waliambulia sare."Ujue sisi tulikuwa tunawasoma dakika 45 za mwanzo ndo maana umeona kipindi cha pili tumerudi kwa kasi," alisema.Aliongeza, kitendo cha mwamuzi wa mchezo huo kutoa kadi nyingi za njano,huenda zikawagharimu kwa namna tofauti kutokana na michezo migumu iliyopo mbele yao."Kadi zitatugharimu sana, mbele kuna michezo migumu, unakuta mchezaji amepata kadi kizembe halafu ni muhimu na anahitajika kwenye michezo mingine sasa anapokosekana kwa adhabu ya kadi hapo ndio inatugharimu,” alisema. | 4 |
JUMLA ya watoto 47 wamezaliwa katika Halmashauri ya Jiji la Arusha katika siku ya mkesha wa kuzaliwa kwake Yesu Kristo usiku wa kuamkia jana, Desemba 25, mwaka huu.Akizungumza na gazeti hili, Daktari Mfawidhi wa Hospital ya Rufaa ya Mount Meru mkoani Arusha, Dk Shafii Msechu alisema katika hospitali hiyo jumla ya watoto 29 walizaliwa wakiwemo wa kiume 17 na watoto wa kike 12. Alisema watoto wote na wazazi wao wako salama. Mganga Mkuu katika Kituo cha Afya cha Kaloleni, Anna Kimaro alisema katika kituo hicho watoto wawili walizaliwa ambao wote ni watoto wa kike.Mkunga katika Kituo cha Afya Ngarenaro, Felista Bwire alisema katika kituo hicho jumla ya watoto watano walizaliwa, wakiwamo wa kiume wawili na wa kike watatu. Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Levolosi, Edward Feksi jumla ya watoto 11 walizaliwa mkesha wa sikukuu ya Krismasi, wakiwemo wa kike watatu na wa kiume wanane. Feksi alisema kuwa mzazi wa mtoto mmoja alijifungua kwa operesheni na wazazi wa watoto wengine walijifungua kawaida, salama na waliruhusiwa jana kwenda majumbani kwao. | 3 |
KUALA LUMPUR, MALAYSIA BINGWA wa mbio za magari Lewis Hamilton ‘Langalanga’, juzi usiku alijikuta akipoteza matumaini ya ubingwa wa Malaysia Grand Prix, baada ya mashine ya gari lake la Kampuni ya Mercedes kuharibika na kushindwa kuendelea na mashindano hayo. Daniel Ricciardo ndiye aliyekuwa bingwa wa michuano hiyo, huku Hamilton akishika nafasi ya pili. Mshiriki mwingine, Nico Rosberg, alimaliza akiwa nafasi ya tatu na pointi 23, huku akibakiwa na mizungu mitano iliyomfanya apoteze pointi 125. Ricciardo ambaye ni bingwa wa mbio hizo, alimshinda Max Verstappen wa Kampuni ya Magari ya Red Bull. Baada ya mbio hizo, Hamilton alilalamika kuhusu Kampuni ya Mercedes kushindwa kumpa gari lenye mashine ya uhakika ambayo lingeweza kumudu mikiki ya wapinzani wake. “Swali langu kwa Mercedes ni, inakuaje tunatengeza mashine nyingi lakini ya kwangu ni miongoni mwa zilizoshindwa kuonesha ubora mwaka huu? “Ni lazima nipate jibu la tatizo hili kwa sababu halikubaliki, tunapambana ili kuwa mabingwa, kwa nini mashine yangu tu ishindwe na ionekane si sahihi kwa ajili yangu,” alihoji Hamilton. Hamilton alikuwa na matarajio makubwa ya kushinda mbio hizo ambazo zilionekana kuwa na ushindani mkali kabla ya kuanza kusumbuliwa na mashine ya gari lake. | 4 |
Alitoa mwito huo jana wakati akifungua semina ya siku tano juu ya mafunzo ya kuingia makubaliano na mikataba kwenye sekta ya madini kwa wanasheria wa sekta ya umma kutoka nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.Katika mkutano huo ulioanza jana jijini Dar es Salaam, Pinda alisema wanasheria wanapaswa kujali wananchi walio masikini kwa sababu wao hawana fursa ya kuingia kwenye vikao kama vyao na kutoa sauti juu ya kile wanachokitaka.“Licha ya umasi kini wao, wanaishi juu ya ardhi ambayo chini yake kuna utajiri tele wa madini na rasilimali nyingine. Ninawasihi sana muwafikirie watu hawa kabla ya kufanya uamuzi wowote,” alisisitiza.Alisema ili jambo hilo liweze kufanikiwa ni lazima, wanasheria kama wadau wa mwanzo kabisa, wakubali kukataa kupokea fedha chafu na vishawishi kutoka kwa wawekezaji na siku zote waweke uzalendo mbele kwa maslahi ya nchi zao.Alisema rasilimali za a Afrika hazijaleta maendeleo kwa wakazi wake kwa sababu wanaofaidika ni kampuni kubwa kutoka nje na watu wachache wenye nafasi huku walio wengi wakiambulia patupu.Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, ni theluthi moja ya mikataba ya uchimbaji madini inayofaidisha bara zima la Afrika ikilinganishwa na faida ambayo bara la Amerika Kusini inanufaika nalo.Ili kuepukana na hali hiyo, Waziri Mkuu alisema umefika wakati wa kukataa kutoa misamaha ya kodi kwa kampuni za kimataifa na kuhakikisha zinalipa kodi katika kila nchi husika ya Afrika Mashariki.Alisema umefika wakati wa kuhakikisha Serikali za nchi husika zinaweka sera madhubuti na miongozo ya kisheria itakayohakikisha mikataba inayoandaliwa kwa ajili ya utafutaji na uendelezaji wa madini na rasilimali zake inazinufaisha nchi kwanza.Akimkaribisha Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema sekta ya madini ni mojawapo ya sekta zinazokua kwa haraka nchini lakini inachangia chini ya asilimia moja ya ajira zote nchini. Washiriki wa mkutano huo ni kutoka Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Tanzania. | 5 |
MWANDISHI WETU-Dar es Salaam RAIS Dk. John Magufuli ametembelea na kuweka shada la maua
katika eneo la mashujaa (Heroes Acre) waliopigania ukombozi wa Namibia, lililopo
nje kidogo ya Jiji la Windhoek nchini humo. Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya
Rais, Ikulu, Gerson Msingwa, ilieleza kuwa katika eneo hilo wamezikwa mashujaa
wa ukombozi wa Namibia ambao baadhi yao walipata mafunzo katika kambi ya Kongwa
nchini Tanzania. Wengine walikuwa maofisa wa Chama cha SWAPO ambao ofisi zao
zilikuwa Dar es Salaam na viongozi wakuu walioendesha mapambano wakiwa nchini
hapa. Baadhi ya mashujaa waliozikwa katika eneo hilo ni Ndimo
Hamaambo, Peter Nanyemba, Theo-Ben Gurirabo na Toiro ya Toire. Rais Magufuli aliongozana na mwenyeji wake Rais wa Namibia,
Hage Geingob. Baada ya kutembelea eneo hilo, Rais Magufuli alitembelea
kiwanda cha nyama cha Kampuni ya Meatco kilichopo Windhoek. Akiwa kiwandani hapo, alielezwa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa
kiwanda hicho, Jannie Breytenbach kuwa wana uwezo wa kuchinja ng’ombe 630 kwa
siku, wameajiri wafanyakazi 650 na kwamba wapo tayari kushirikiana na Tanzania
kuanzisha viwanda vya nyama. Rais Magufuli alisema Tanzania ni nchi ya pili kwa idadi
kubwa ya mifugo barani Afrika na ameikaribisha Meatco kuja kuwekeza nchini. Katika ziara hiyo, ameongozana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi,
Luhaga Mpina, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi. Kabla ya kuondoka nchini Namibia kwenda Zimbabwe ambako
anakwenda kufanya ziara rasmi ya kitaifa kwa mwaliko wa Rais wa Zimbabwe, Emmerson
Mnangagwa, Rais Magufuli alikutana na kufanya mazungumzo na Rais mstaafu wa pili
wa Namibia, Hifikepunye Pohamba jijini Windhoek. | 3 |
OFISA Mazingira kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Magori Wambura, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam akikabiliwa na mashitaka mbalimbali ya uhujumu uchumi.Moja ya mashitaka anayoshitakiwa nayo ni kughushi sahihi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba na kujipatia Sh milioni 160 kwa njia za udanganyifu.Wambura (38), ambaye ni mkazi wa Ukonga Bombambili, ameunganishwa katika kesi hiyo inayowakabili maofisa wengine watano wa NEMC, ambao walifikishwa mahakamani hapo mwezi uliopita.Maofisa hao ni Deusdedith Katwale (38), Lilian Laizer (27), Luciana Lawi (33), Edna Lutanjuka (51) na Mwaruka Miraji (42). Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Auguistina Mbando, Wambura hakuruhusiwa kujibu chochote dhidi ya mashitaka yanayomkabili.Mashitaka mengine yanayomkabili Wambura na washitakiwa wengine ni pamoja na kula njama kutenda kosa la kughushi, kuwasilisha hati bandia na kusababisha hasara kwenye mamlaka husika.Hakimu huyo alimweleza Wambura kuwa mashitaka yanayomkabili yanaangukia katika Sheria ya Uhujumu Uchumi, hivyo kuifanya mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kuisikiliza, mpaka itakavyoamriwa vinginevyo na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP). Kutokana na hatua hiyo, Hakimu aliamuru mshitakiwa huyo kubaki mahabusu mpaka Novemba 28, kesi hiyo itakapotajwa kwa vile upelelezi, kwa mujibu wa upande wa mashitaka, bado haujakamilika.Mwanasheria wa Serikali Neema Mbwana alidai mbele ya mahakama hiyo kuwa kati ya Septemba 27, 2016 na Aprili 6, 2018, jijini Dar es Salaam, washitakiwa kwa pamoja walikula njama kutenda kosa la kughushi. Imeelezwa kuwa Oktoba 17, 2017, maofisa wa NEMC kwa nia ya kudanganya walighushi cheti cha tathmini ya mazingira wakidai kuwa kilikuwa halisi wakati si kweli.Mahakama ilielezwa na upande wa mashitaka kuwa katika kipindi hicho hicho jijini Dar es Salaam, maofisa hao walighushi sahihi ya Makamba kwenye cheti hicho, wakidai kuwa ilikuwa ni sahihi yake hali wakijua kuwa ni uongo.Oktoba 2017, Makao Makuu ya NEMC jijini Dar es Salaam, wakati akijua ni udanganyifu, Edna anadaiwa kuwasilisha cheti hicho kwa Deogratius Chacha akidai kuwa kimetolewa na NEMC, wakati si kweli. Kwa mujibu wa upande wa mashitaka, kati ya Septemba 27, 2016 na Aprili 6, 2018, jijini Dar es Salaam, washitakiwa wote walijipatia Sh milioni 160 kutoka kampuni ya PMM Estate (2001) LTD, kwa kudanganya kuwa wangefanya tathimini ya mazingira na kumpatia cheti kinachohusika wakati si kweli. | 3 |
Mashabiki wa timu hiyo walionekana kuchukizwa na kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Yanga katika pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara lililopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Akizungumza na gazeti hili, Mayanja alisema yeye binafsi ameumizwa na matokeo hayo, lakini hakuna namna ya kuyabadilisha na kitu muhimu kwao ni kujipanga kuhakikisha wanapata matokeo mazuri mechi zao zinazofuata ili kuendelea kuwepo kwenye mbio za ubingwa.“Binafsi ninaumia kila ninapoukumbuka huo mchezo, lakini huu ni mpira tunapaswa kusahau ili kuweka mawazo yetu kwenye mchezo unaokuja, ili tuweze kufanya vizuri kwa sababu una umuhimu na bado hatujatoka kwenye mbio za ubingwa,” alisema Mayanja.Kocha huyo raia wa Uganda aliyetua Simba akitokea Coastal Union ya Tanga, alisema baada ya mchezo huo kazi yake kubwa inayomkabili kwa sasa ni kuwarudisha wachezaji wake mchezoni na kuhakikisha wanazingatia kile anachowafundisha ili waweze kuendeleza kasi waliyoanza nayo wakati alipoanza kuifundisha timu hiyo.Alisema wachezaji wake wameumizwa na kipigo hicho na anajaribu kuzungumza nao ili warejeee katika hali ya kawaida.Kipigo cha mabao 2-0, Simba ilichokipata Jumamosi kutoka kwa Yanga ni cha kwanza kwa Mayanja baada ya kuiongoza timu hiyo kushinda mechi sita mfululizo tangu akabidhiwe mikoba ya kuinoa timu hiyo katikati ya Januari mwaka huu.Simba Jumapili itashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza na Singida United katika mchezo wa kuwania Kombe la Shirikisho. | 4 |
Mke wa Tito Machibya Maarufu kwa jina la Nabii Tito, Agnes Miri (36), leo ameweka kambi Kituo Kikuu cha Polisi mkoani Dodoma, akishinikiza mume wake atolewe kwani amekuwa akiishi maisha magumu. Nabii huyo ambaye jana alijaribu kujiua kwa kujikata na wembe tumboni na kushonwa nyuzi 25, akiwa chini ya Jeshi la Polisi bado anashikiliwa na jeshi hilo. Akiwa na watoto wake watatu katika viunga vya polisi, mke wa nabii huyo ambaye amekuwa akionekana na mume wake wakicheza muziki na kunywa pombe, ameiambia Mtanzania Digital, anaomba jeshi hilo limwachie mume wake kwani maisha yamekuwa magumu kwake. Amesema yeye na watoto wake wanaumwa ugonjwa wa kuhara na kutapika ambapo kutokana na mume wake ambaye ndiyo mwangalizi wa familia kushikwa na polisi hana mtu wa kumsaidia. “Maisha yangu ni magumu mimi naliomba Jeshi la Polisi pamoja na Serikali imwachie mume wangu kwani yeye ndiyo kila kitu kwangu ninavyokwambia hapa tangu jana sijatia kitu chochote tumboni na hawa watoto unawaona wanalia tu sababu ya njaa na pia wanaumwa wanatapika na kuharisha. “Asubuhi jirani alinipa buku (Sh 1,000) ndiyo nimeitumia kama nauli kuja hapa kituoni sasa mimi sitoki hadi wamtoe mume wangu wamtoe yeye ndio kimbilio langu, amesema. Pamoja na mambo mengine, Agnes amehoji kama Hospitali ya Magonjwa ya akili ya Mirembe wamempima na kugundua Nabii Tito ana matatizo ya akili ni kwanini waendelee kumng’ang’ania. “Wamesema yule ni kichaa sasa kwanini wanamng’ang’ania wananifanya mimi maisha yangu yawe magumu,” amesema | 3 |
WADAU wa utalii wametabiri kuwa Wilaya ya Kisarawe itakua kimapato na kupata umaarufu kitaifa na kimataifa kutokana na utalii baada ya kufunguka kwa Barabara ya Dar es Salaam-Kisarawe hadi Hifadhi ya Taifa ya Mwalimu Julius Nyerere.Chama cha Watembeza Watalii Kusini mwa Tanzania (STTGS) kupitia kwa katibu wake, Dioniz Kazungu kimesema vivutio vya utalii vilivyomo wilayani Kisarawe katika Mkoa wa Pwani vitafahamika na wakati huohuo safari za kwenda katika hifadhi hiyo zitakuwa nyingi ikizingatiwa wilaya ipo karibu na Jiji la Dar es Salaam.“Kutoka Dar es Salaam hadi gati la kuingia hifadhi ya Mwalimu Nyerere kwa kupitia barabara hii, takribani Kilometa 180 ni saa nne. Hii ina maana sasa badala ya kufanya safari zile fupi za Mikumi, ambayo iko mbali, sasa safari nyingi zitakuwa kwa Mwalimu Nyerere National Park,” alisema Kazungu.Alisema hayo hivi karibuni baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo kukutana na waongoza watalii na wadau wengine wa sekta ya utalii kwa lengo la kutangaza rasmi fursa zitokanazo na barabara hiyo.Katika mkutano huo ambao waongoza watalii walifanya ziara kwenye vivutio mbalimbali vya utalii wakiongozwa na Ofisa Utalii wa wilaya, Kennedy Muhoza, Kazungu aliomba serikali kufanyia matengenezo sehemu korofi ambazo kipindi cha mvua hazipitiki.Akipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuendeleza utalii Kusini na Magharibi ya Tanzania hususani kwenye hifadhi hiyo mpya ya Mwalimu Nyerere, Kazungu alisema “tunaomba ione umuhimu wa kutengenza kwa kiwango cha lami angalau mpaka gati la Mtemere ili kuongeza ufanisi wa kazi yetu.”Kiongozi huyo wa waongoza watalii alisema hifadhi hiyo itakuwa ni ya kipekee na yenye mandhari nzuri ya kuvutia itakayoungana na hifadhi nyingine zilizotawanyika kikanda.Alitaja kanda hizo na idadi idadi ya hifadhi kwenye mabano ni Kaskazini (tano), Magharibi (saba), Mashariki (tatu) na Kusini zipo tatu.Akitaja fursa za uwekezaji katika utalii, Ofisa Utalii wa Wilaya, Muhoza, alisema Kisarawe ni wilaya iliyo jirani na hifadhi ya Mwalimu Nyerere (kilometa 152).Pia iko karibu na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) na Jiji la kibiashara la Dar es Salaam kwa takribani kilometa 15. | 5 |
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika mkoa wa Dodoma imevitaka vyuo vikuu vyote mkoani humo kuhakikisha huduma zinazotolewa ndani ya vyuo ziwe zimesajiliwa, zinalipiwa kodi na zinatumia Mashine za Kielektroniki (EDF).Akitoa taarifa ya utendaji wa TRA katika Mkoa wa Dodoma kwenye kikao cha wajumbe wa Jukwaa la Wadau wa Kodi mkoani humo, Meneja wa TRA Mkoa wa Dodoma, Kabula Mwemezi alisema huduma zinazotolewa vyuoni humo zinatakiwa kusajiliwa.Alizitaja huduma zinazotakiwa kusajiliwa ni za kumbi za mikutano, huduma za wapishi, wapambaji, hosteli binafsi na nyingine nyingi.Mwemezi pia aliwaomba wakurugenzi wa halmashauri zote nane za mkoa huo za Bahi, Kondoa Mji na Vijijini, Chemba, Kongwa, Mpwapwa, Jiji na Chamwino kuhakikisha wana orodha ya wazabuni, wenye hati za udhibitisho wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na EDF.Alisema pia halmashauri hizo zihakikishe zinazuia na kuwasilisha kodi ya zuio kwa kila malipo yanayofanywa na ofisi za wakurugenzi.Alimwomba Ofisa Elimu Mkoa kusimamia shule zote za binafsi mkoani humo zilizosajiliwa na kuhakikisha zinatumia mashine za EDF katika makusanyo mbalimbali wanayofanya.“Nawaomba maofisa ushirika wote mkoani kuhakikisha wanaipatia mamlaka ya mapato orodha ya Vyama vya Akiba na Mikopo (Saccos) na vyama vya ushirika vilivyosajiliwa katika halmashauri zote,” alisema.Mwemezi pia aliwaomba wakuu wa vikosi vya Jeshi, Wakala wa Barabara (Tanroads) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (Tarura), kutoa kwa mamlaka hiyo orodha ya wazabuni wanaofanya kazi nao, ili waoneshe vithibitisho vya kodi VAT, EDF, kodi ya zuio.Akifungua kikao cha wajumbe wa Jukwaa la Wadau wa Kodi Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge alitaka TRA kuongeza mapato wakishirikiana na taasisi na wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari.Alisema jukwaa hilo ni muhimu kuhakikisha Mkoa wa Dodoma unaendeleza rekodi ya kuongoza katika kukusanya mapato kwa wingi kupitia Halmashauri ya Jiji au kupitia TRA.Aliwataka wadau kushirikiana na TRA kufikia malengo waliyoweka hasa kipindi cha pili cha mwaka huu hadi kufikia Juni mwaka huu na kuvuka malengo ya kukusanya Sh bilioni 67.Katika kuhakikisha mikutano ya Jukwaa hilo inafanyika bila kukosa, pia lilimchagua Makamu wa Mwenyekiti, Deus Nyabiri ili kumsaidia Mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa katika kuendesha mikutano ya jukwaa hilo inayofanyika mara mbili kwa mwaka.Mkoa wa Dodoma hadi kufikia Desemba 31, mwaka jana umesajili walipa kodi 106,847 ambapo kati yao, wafanyabiashara 83,0004 ni hai, wanaobaki si hai, haijulikani wanakofanyia. | 5 |
POLISI mkoani Morogoro imefanikiwa kuwatia mbaroni watu watatu akiwemo Filbert Katabazi (35) dalali wa magari mkazi wa Makongo Dar es Salaam, aliyekuwa akisakwa kwa muda mrefu na Polisi kwa tuhuma za wizi wa mitandao na utapeli.Mtuhumiwa huyo anadaiwa kufunguliwa kesi mbalimbali za tuhuma za wizi wa mitandao na utapeli na kujipatia fedha Sh milioni 4.9 zilizohamishwa kutoka akaunti ya Amos Mniko iliyopo Benki ya NMB. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa alisema jana kuwa tukio hilo lilifanyika Oktoba 25, mwaka huu, majira ya saa mbili usiku ambapo mlalamikaji Mniko alifika kituo cha Polisi Morogoro na kutoa taarifa za kuibiwa fedha Sh milioni 4.9 kutoka katika akaunti yake ya NMB na kuhamishiwa akaunti nyingine ya NMB.Alisema Oktoba 23, mwaka huu, mlalamikaji alihamisha fedha Sh 710,000 kutoka akaunti yake ya NMB na kumtumia mke wake kwa M-Pesa lakini hakupata mrejesho wa muamala kutoka NMB. Alieleza kuwa aliamua kupiga simu kwenda NMB huduma kwa wateja NMB 0786800008 ambayo aliikuta katika kadi yake na kupokewa na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mfanyakazi wa NMB ambaye ni Filbert Katabazi mkazi wa Dar es Salaam.Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi huyo mlalamikaji alimjulisha kuwa anahitaji apate taarifa ya fedha aliyotuma, ndipo alipopewa maelekezo kadhaa ya kufanya hatimaye akashtuka kuona Sh milioni 4.9 zimehamishwa kutoka katika akaunti yake. Kamanda Polisi mkoa alisema, upelelezi wa kina ulifanyika na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili ambao ni Hans Bakari na Hamis Msangi waliohamishiwa fedha na Katabazi ambaye anatumia namba ya NMB huduma kwa wateja kuwaibia wateja wa NMB.“Mtuhumiwa huwadanyanga vijana kuwa anawatafutia ajira kisha kuwafungulia akaunti NMB chapchap na kuchukua kadi zao akidai kwenda kuwafanyia uhakiki wa daftari la mishahara, akaunti ambazo hutumika kufanyia uhalifu huo wa kimtandao,” alisema Kamanda Mtafungwa. Kamanda alisema juhudi za kuwakamata watuhumiwa wengine anaoshirikiana nao ambao majina yao yamehifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi zinaendelea. | 3 |
SERIKALI imeyataka mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na taasisi mbalimbali, zinazojihusisha na utetezi wa haki ya mtoto, kuongeza jitihada za mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa ya ngono na unyanyasaji, vinavyozidi kuongezeka mkoani Arusha.Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Hargeney Chitukuro alisema hayo jana alipokuwa akizindua kampeni ya siku 16 ya kupinga vitendo vya rushwa ya ngono kwa mwanamke, inayoendelea jijini hapa.Alisema mashirika hayo, yakiongeza juhudi kwa kushirikiana na serikali, vitendo hivyo vitapungua ama kumalizika. Chitukuro alitolea mfano wa baadhi ya shule binafsi mkoani hapa kuwa walimu wamekuwa wakidai rushwa ya ngono kwa wanafunzi wa kike, lakini wamiliki wa shule hizo, hawachukui hatua za kisheria.Badala yake, wamiliki hao wa shule wamekuwa wakiacha matukio hayo yamalizike kifamilia. “Tatizo la rushwa ya ngono ni la kitabia au kimfumo na limeongezeka sana hapa Arusha linafanywa kwa siri na linawajengea hofu ya kujieleza hadharani au kutoa ushahidi kwa wahusika, hivyo tunayataka mashirika yanayojihusisha na haki za watoto kusaidia kufichua,” alisema.Wakizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo ya kupinga ukatili wa wanawake na watoto, iliyofanyika katika Shule ya Msingi Moshono jijini Arusha, ambayo kilele chake ni kesho, Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Sasa Foundation, Jovita Mlay alisema rushwa hiyo bado ipo.Alisema pamoja na wao kupiga kelele dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kwa mtoto na rushwa ya ngono, bado jamii imekuwa na mwamko mdogo wa kutoa ushirikiano hasa ushahidi mahakamani.Kaimu Ofisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Arusha, Denisi Mndee alisema waathirika wengi wa matukio ya ukatili ni watoto na wanawake. Kwamba takwimu za mwaka 2016/17 zinaonesha kuwa matukio yaliyoripotiwa ni 1,437 na mengi ni ya ubakaji, mimba za utotoni. | 3 |
Na ARODIA PETER-DAR ES SALAAM
JUKWAA la Katiba Tanzania (JUKATA) limesema lina matumaini makubwa kwamba Waziri mpya wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi atawezesha kukamilishwa kwa mchakato wa Katiba mpya ambao umekwama.
Jukwaa hilo limesema kupitia kwa Profesa Kabudi, Watanzania watapata Katiba mpya ambayo waliitolea maoni kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba na waziri huyo alikuwa mjumbe wake.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Jukwaa hilo Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa JUKATA, Hebron Mwakagenda alisema uzoefu wa Profesa Kabudi unahitajika wakati huu ambao mwelekeo wa kupatikana kwa Katiba mpya haupo bayana.
“Kutokana na ushiriki wake katika mchakato mzima wa kukusanya maoni ya Watanzania akiwa Kamishna wa Tume, ni matumaini ya JUKATA na Watanzania kwa ujumla kwamba msomi huyo atawezesha kukamilisha mchakato wa Katiba mpya itakayokuwa imekidhi vigezo, mahitaji na matumaini ya walio wengi.
Mkurugenzi huyo wa JUKATA alisema kwa kutambua mchakato wa Katiba mpya ulisimama wenyewe zipo changamoto kuu mbili ambazo zinatakiwa kutafutiwa ufumbuzi kwanza.
Alizitaja changamoto hizo kuwa ni kurekebisha Sheria ya mMbadiliko ya Katiba Na. 8 ya 2011 na marekebisho yake pamoja na Sheria ya Kura ya Maoni ya 2013.
Alisisitiza kuwa ni vema marekebisho hayo yalenge kuhuisha vifungu vilivyopitwa na wakati.
Jukwaa la Katiba limeishauri Serikali kutoa taarifa rasmi kwenye Gazeti la Serikali kuufanya mchakato huo kuwa hai.
Mwakagenda alisema kabla ya kufanya marekebisho yoyote ya sheria kwa sasa ni vema wananchi wapate fursa ya kujadili kwa kina masuala ya msingi ambayo lazima yaingizwe kwenye marekebisho hayo.
“Tunashauri katika Bunge hili la bajeti 2017/2018 waziri apeleke miswada ya marekebisho ya sheria zinazosimamia mchakato wa Katiba mpya.
“Kwa kuwa Tume ya Mabadilio ya Katiba haipo, tunashauri kiundwe chombo maalum kusimamia hatua zilizobaki,” alisema.
Wiki iliyopita, akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Profesa Kabudi alisema Serikali itaanza kazi ya kurekebisha sheria kukamilisha upatikanaji wa Katiba mpya. | 3 |
KATIKA kipindi cha miaka minne tangu kuanzishwa kwake, mpango wa elimu bure nchini umezaaa matunda baada ya wanafunzi milioni tatu kusajiliwa. Kati ya hao, kwa upande wa shule za msingi waliosajiliwa ni wanafunzi milioni 2.4 na sekondari 600,000.Pia, serikali imeanza kuifanyia mapitio Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, ambayo wadau mbalimbali wakiwamo wabunge watapata fursa ya kutoa maoni yao. Hayo yamebainishwa bungeni jana na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (Chadema).Katika swali lake, Lyimo alisema walimu wa shule za msingi, wanafundisha mitaala sawa na awali, wakati awali ni za msingi sana na ndipo mtoto anapata elimu ya muhimu sana hivyo wanapaswa kufundishwa namna ya kulea watoto, je, serikali haioni umuhimu wa kuwapa kipaumbele walimu hao wa shule za awali. Akijibu swali hilo, Ole Nasha alisema katika kipindi cha miaka minne, serikali imeongeza upatikanaji wa elimu mfano kwa shule za msingi kutoka wanafunzi milioni 8.2 kwa mwaka 2015 hadi milioni 10.6 kwa mwaka 2019.“Hivyo ndani ya miaka minne tumeongeza wanafunzi milioni 2.4 kwa shule za msingi miaka hiyo,” alisema.Aidha, alisema kwa upande wa shule za sekondari, wameongeza wanafunzi milioni 1.7 kwa mwaka 2015 hadi wanafunzi milioni 3.3 mwaka mwaka 2019..“Hivyo ndani ya miaka minne tuna ongezeko la wanafunzi wapya zaidi ya 600,000 na ni matunda ya elimu bila malipo,” alisema Ole Nasha.Alifafanua kuwa kwa sasa wanarejea mitaala ili iendane na elimu ya sasa na mifumo inafanyiwa kazi na kwenye sera maoni yatakayotokewa, ndio yatafanyiwa kazi ili kuwepo mitaala bora zaidi. Awali katika swali la msingi, Lyimo alisema mfumo wa elimu umekuwa ukilalamikiwa na kukosolewa, na kuhoji kama serikali imefanya utafiti wowote kuona kama lawama hizi zina mashiko au la.Akijibu swali hilo, Ole Nasha alisema serikali imeanza kuifanyia mapitio Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014, ambapo katika mchakato huo wadau mbalimbali wakiwemo wabunge watapata fursa ya kutoa maoni yao.Alifafanua kuwa serikali imekuwa ikipokea maoni mbalimbali ya wadau kuhusu Mfumo wa Elimu nchini na kuyafanyia kazi. Pamoja na hivyo, kupitia Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu 2016/17 – 2020/21, wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu imekuwa ikifanya ufuatiliaji na kupokea mrejesho juu ya Mfumo wa Elimu nchini.Alifafanua kuwa kufuatia mrejesho huo hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa kwa lengo la kuboresha Elimu. | 3 |
NORA DAMIAN Na AZIZA MASOUD
-DAR ES SALAAM
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, jana lilikwenda kufanya upekuzi ofisini kwa mfanyabiashara maarufu, Yusuph Manji, baada ya kufanya zoezi kama hilo juzi nyumbani kwake.
Manji pamoja na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, juzi waliripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam ikiwa ni wito wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye aliwataja katika orodha ya watu 65 wanaojihusisha na dawa za kulevya.
Hii ni mara ya pili polisi kufanya zoezi la upekuzi kwa Manji ambapo kwa mara ya kwanza walifanya zoezi hilo juzi nyumbani kwake pamoja na kwa askofu huyo.
Taarifa toka ndani ya Jeshi la Polisi zinadai kuwa Manji alitoka kituoni hapo akiwa ameongozana na maofisa kadhaa wa polisi na msafara wao kuelekea moja kwa moja zilipo ofisi zake.
Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro, kuthibitisha taarifa hizo alijibu kwa kifupi: “Nipo kikaoni nipigie baadaye.”
Mwandishi alimpigia tena saa 1:00 usiku na alipoulizwa juu ya taarifa za mfanyabiashara huyo kuondolewa kituoni hapo, maongezi yalikuwa kama ifuatavyo:-
Mwandishi: Tumepata taarifa kuwa Manji ameondolewa hapo Central akiwa na polisi.
Kamanda Sirro: Ameenda wapi?
Mwandishi: Kuna taarifa kwamba ameenda kupekuliwa ofisini kwake na maofisa wa polisi.
Kamanda Sirro: Mimi sijui bwana.
Baada ya kutoa jibu hilo alikata simu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mchana, Sirro alikiri kuendelea kuwashikilia kituoni hapo, Manji na Gwajima.
Hata hivyo, jana Sirro hakuwa tayari kueleza walikokuwa wamewapeleka Manji na Gwajima juzi baada ya kuonekana wakiondoka kituoni hapo chini ya ulinzi mkali.
Wakati Sirro akikataa kuweka wazi hilo, taarifa ambazo gazeti hili limezipata toka kwa watu wa karibu na Manji na Gwajima, zinaeleza kuwa walielekea kwenda kufanya upekuzi majumbani mwao.
“Katika yale majina 65 Manji na Gwajima waliripoti jana (juzi) na upelelezi uliendelea mpaka usiku, walilala na hadi sasa wako mahabusu upelelezi unaendelea kufanyika.
“Kuna vitu ambavyo vinaashiria tuendelee kupeleleza, baada ya hapo wanaweza kufikishwa mahakamani au wasifikishwe…ni mapema mno kusema,” alisema Sirro.
Katika hatua nyingine, Sirro alisema pia wanawashikilia watu 11 baada ya kukamatwa wakiwa na kete 38 zinazodhaniwa kuwa ni za dawa za kulevya.
Pia alisema katika operesheni hiyo wamekamata magunia sita ya bangi.
Walioripoti jana
Hadi MTANZANIA Jumamosi linaondoka kituoni hapo majira ya mchana jana, waliokuwa wameripoti ni Mbunge Mstaafu wa Kinondoni, Idd Azzan na mmoja wa wamiliki wa Casino iliyoko ndani ya Hoteli ya Sea Cliff.
Azzan aliwasili kituoni hapo saa 3:06 asubuhi kwa gari aina ya Jeep yenye rangi nyekundu huku pia akiwa ameongozana na watu wengine wawili.
Saa 4:27 asubuhi mmoja wa wamiliki wa Casino iliyoko ndani ya Hoteli ya Sea Cliff aliwasili kituoni hapo akiwa kwenye gari aina ya Toyota Alifat yenye namba T 356 DHU.
Mtu huyo ambaye alionekana kuwa na mwili mkubwa na umri uliokwenda kidogo, alishuka kwenye gari huku akisaidiwa na watu wengine wawili na baada ya hapo mmoja wa wasaidizi wake alizunguka katika buti ya gari na kuchukua kiti maalumu cha kukalia na kuingia nacho ndani ya kituo cha polisi.
Hata hivyo, idadi ya watu waliofika kituoni hapo kuhojiwa ni wanne tu kati ya 65 waliotajwa na Makonda.
“Waliotajwa waje timu ya upelelezi inawasubiri wahojiwe na wanaoonekana wanahusika tutaendelea nao na wasiohusika tutawaachia.
“Hakuna sababu ya kuwa na woga wowote kwa sababu watu wanapiga simu sana na wengine wanatuma ndugu zao waje kuniona, kama umetajwa na unajua uko clean (msafi) huna tatizo lolote njoo watakuhoji wakiona huhusiki watakuachia,” alisema Sirro.
Alisema timu ya upelelezi iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa inayohusisha vyombo vya dola na vingine ina lengo la kuhakikisha kwamba upelelezi unakuwa wa haki kwa wanaotuhumiwa.
“Mpaka sasa waliofika ambao nimewaona wako wanne na wengine wanaendelea kuja lakini sitaweza kutaja majina yao. Anayefika si lazima akae ndani tukikuhoji tukafuatilia baadhi ya mambo ya msingi (Preliminary investigation) tunaweza kujua tuna mtu wa aina gani na tutajua kama unabaki au unatoka.
“Kama kuna vitu ambavyo vitatuonyesha kwamba kuna dalili fulani tutabaki na wewe kwa lengo la kutaka kuthibitisha ukweli wa yale ambayo upelelezi unakuwa umeonyesha,” alisema Sirro.
Alisema wako baadhi ya watu walioshindwa kuripoti na mawakili wao wametoa taarifa, lakini hakuwa tayari kutaja idadi wala majina ya watu hao.
Hali ilivyokuwa
Idadi ya watu nje ya kituo hicho cha polisi jana iliongezeka tofauti na siku zilizopita.
Wingi huo ulimlazimisha Kamanda Sirro kuingilia kati na kutishia kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya machozi. | 3 |
ELIYA MBONEA-ARUSHA MIILI ya watu watatu waliofukiwa na gema katika machimbo ya moram
yaliyopo Moshono Kata ya Moivaro jijini Arusha, imeipolewa huku ikiwa
imeharibika kwa kutoboka macho na kukatika mikono. Gema hilo lilianguka jana asubuhi na juhudi za uokoaji zilianza saa 2
asubuhi ambapo hadi majira ya mchana kwa vikosi vya askari polisi, zimamoto
vikishirikiana na wananchi walifanikiwa kuipata miili hiyo na gari
lililofunikwa gema hilo. Katika tukio hilo pia watu wawili walijeruhiwa na kukimbizwa
Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru. Kukatika kwa ngema hilo kunadaiwa kusababishwa na mvua
zilizonyesha jana usiku katika baadhi ya maeneo ya mji wa Arusha. Mwaka 2013
katika machimbo hayo gema lilianguka na kuua watu 13. Mkuu wa wilaya ya Arusha, Fabian Daqarro alisema wanaendelea na juhudi
za kuokoa miili hiyo na hawata simama mpaka wafanikiwe kuitoa kwenye vifusi.
“Miili mitatu imetolewa na watu wawili waliojeruhiwa wamekimbizwa
Hospitali ya Mount Meru, tupo hapa kuhakikisha miili ya waliofunikiwa
inapatikana,” alisema DC Daqarro na kuongeza: “Ngema hili ni kubwa limeanguka baada ya mvua kunyesha usiku wa
jana,” alisema. Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan
Shana, alisema kwa kushirikiana na vikosi vya Jeshi la Zimamoto, Polisi na
Jeshi la Wananchi watahakikisha zoezi linafanikiwa. Naye Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro, alisema taarifa hizo
walizipata mapema asubuhi na wakatoa mashine ya Jiji kwa ajili ya kusaidia
uokozi. Alisema Halmashauri ya Jiji huchukua ushuru wa Sh 20,000 kwa
kila gari linaloingia kuchukua Moramu huku ushuru mwingine ukichukuliwa na
Wizara ya Madini. Lema Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), akizungumzia
eneo la tukio alisema suluhisho la mgodi huo si kuufunga badala yake mamlaka
husika zitafute ufumbuzi wa kudumu. “Hapa kuna familia zinategemea machimbo haya kulisha familia na
kujipatia riziki,” alisema Lema. Mchimbaji wa moramu kwenye mgodi huo, Leston Joeli aliliambia
MTANZANIA kuwa hapo ndipo wanapopata riziki za kuendeshea maisha yao ya kila
siku ikiwamo kusomesha watoto wao. “Hapa ndipo riziki ya kula na watoto wetu inapopatikana, tunafanya
kazi Jumatatu Saa 1 asubuhi mpaka Jumamosi 11 jioni. Hili ni tukio la bahati
mbaya, kulikuwa hakuna dalili zozote za hili ngema kuanguka. “Sasa kwa vile watu tayari walikuwa wameshaingia kufanya kazi
chini, lilipodondoka likawafunika wakiwa na gari aina ya Isuzu iliyokuwa
ikipakia moramu,” alisema Joel. Kwa upande wake mpakiaji wa moramu kwenye mgodi huo Apolinary
Amandus alisema hali hiyo huwa inajitokeza pindi kuta za mlima huo zinapopoteza
uimara. Akizungumzia kuhusu tahadhari wanazochukua pindi kunapokuwa na mvua au
hali ya hatari kwenye eneo hilo, dereva wa magari yanayobeba moramu, Geofrey
John, alisema huwa wanapewa tahadhari ya kutokukaribia kwa muda. “Moramu hii inaendesha maisha ya watu, hapa mgodini
tunanunua lori moja kwa Sh 60,000 pamoja na ushuru wake na sisi tunaenda
kuuza kati ya Sh 100,000 hadi 110,000,” alisema John. | 3 |
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein ameeleza kuridhishwa na mafanikio makubwa yaliopatikana Zanzibar chini ya uongozi wake wa Serikali ya Awamu ya Saba, ambao umetimiza miaka tisa.Ameyasema hayo jana Ikulu mjini Zanzibar alipofanya mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Zanzibar (ZBC), Chande Omar Omar, kufuatia kutimiza miaka tisa ya uongozi wake Zanzibar.Katika maelezo yake, Rais Shein alisema kuwa anafurahia miaka tisa ya uongozi wake, kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana hapa Zanzibar, ambayo kwa kiasi kikubwa yametokana na kutekeleza mambo ya msingi ikiwemo kutekeleza Ilani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015 na 2015- 2020.Aliongeza kuwa serikali inatakiwa baada ya kumaliza uchaguzi wake, chama kilichoingia madarakani kitekeleze ahadi zake, jambo ambalo ndilo lililofanywa na Serikali anayoiongoza, ambayo imetekeleza kwa kiasi kikubwa ahadi ilizoahidi ndani ya kipindi cha miaka tisa ya uongozi wake.Aidha, Rais Shein alisema kuwa amefurahi kuona kwamba katika uongozi wake, mafanikio makubwa yamepatikana katika utekelezaji wa MKUZA II alioanza nao na MKUZA III unaondelea hivi sasa.Kwamba serikali anayoiongoza imeendeleza umoja na mshikamano mkubwa wa wananchi wa Zanzibar, kwa kutambua kuwa bila ya kuwepo kwa umoja na mshikamano huo, hapatakuwa na maendeleo endelevu.Alisisitiza kuwa azma ya CCM ni kutekeleza umoja na mshikamano na ndio maana katika kipindi chote cha uongozi wake wa miaka tisa, ulinzi na usalama wa nchi na wananchi wa Zanzibar umeimarika Kwamba serikali zote mbili, ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, zinaendelea kusimamia amani na usalama uliopo nchini.Alisisitiza kuwa ndani ya miaka tisa ya uongozi wake, nchi imekuwa salama.Alieleza kuwa sekta nyingi za maendeleo, zimeimarika katika kipindi cha miaka tisa cha uongozi wake na serikali imetekeleza kwa kiasi kikubwa shughuli za kijamii, zikiwemo huduma za afya, elimu,kuangalia hali za wananchi na shughuli za maendeleo zimeimarika.Alisema kuwa kila sekta imepata mafanikio makubwa sana na kueleza kuwa anajivunia kwa kiasi kikubwa mafanikio hayo, yaliofikiwa katika kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2010-2015 na 2015-2020 pamoja na MKUZA II na MKUZA wa III.Rais Shein ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, alieleza kuwa wananchi wataendelea kuiunga mkono CCM kutokana na juhudi zake za maendeleo na kukuza uchumi .Aliwataka wananchi kuhakikisha miundombinu iliyofanywa na serikali, wanaitunza na kuitumia vizuri.Alieleza umhimu wa kuongeza bidii ili uchumi uendelee kukua kwa kasi na nguvu zaidi kwani alipoingia madarakani kasi ya ukuaji ilikuwa asilimia 4.3 na sasa ni asilimia 7.1, ukuaji huo umetoa mwelekeo vizuri na kuiwezesha Zanzibar kufikia nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2020 huku akieleza dhamira yake kwa kipindi kilichobakia atafanya jitihada ya kuhakikisha kasi ya ukuaji uchumi inafikia asilimia 7.5 mnamo mwezi Juni mwakani.Alieleza kuwa kwa upande wa mfumko wa bei umepungua kwani ulikuwa asilimia 6.1 alipoingia madarakani na hivi sasa umefikia asilimia 3.9 jambo ambalo linaleta utulivu katika mwenendo wa biashara na kuongeza kuwa katika kipindi chake juhudi kubwa zimechukuliwa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara, ujenzi wa skuli za kisasa katika ngazi zote zikiwemo za Maandalizi, Msingi na Sekondari. Kuhusu huduma za afya, alisema zimeimarika kwa kiasi kikubwa, ikilingalishwa na nchi nyingine za Bara la Afrika na hata nje ya bara hilo.Alitoa mfano wa Hospitali za Zanzibar zilivyopandishwa daraja sambamba na kuanzishwa kwa utoaji wa huduma za usafishaji figo, saratani na nyingine za afya.Kuhusu suala la uimarishajai wa sekta ya utalii, alisema kuwa mafanikio makubwa yamepatikana katika sekta hiyo na kuwa lengo lililobainishwa na Ilani la kupokea watalii 500,000 ifikapo mwaka 2020, tayari limeshafikiwa kabla ya wakati huo.Alibainisha kwamba mwaka jana Zanzibar ilipokea watalii 520,809.Alieleza pia kuwepo kwa afya bure, elimu bure, misingi ya utawala bora na haki za binaadamu, uhuru wa kuabudu na uvumilivu wa dini hapa Zanzibar.Hata hivyo, alieleza changamoto zilizopo ikiwemo suala zima la ajira na tayari serikali imeweka mikakati ikiwemo kuweka mifuko maalum ukiwemo ‘Mfuko wa Kuwaewezesha Kiuchumi Wajasiriamali’ na ‘Mfuko wa Vijana’, ambapo kwa ‘Mfuko wa Vijana’ tayari Sh bilioni 46 zimetengwa.Rais Shein alisitiza kuwa amani na utulivu, ndio suala muhimu katika maendeleo ya Zanzibar, hatua ambayo imemfanya abuni mradi wa ‘Zanzibar Salama’ ili usalama uimarike sambamba na kuimarisha sekta ya utalii na mazingira yake. | 3 |
CHRISTIAN BWAYA TULISHAWAHI kujadali nafasi ya dada wa kazi katika malezi. Tuliona kuwa pamoja na unafuu wa huduma zao, wamekuwa wakikabiliana na uhusiano hafifu na waajiri wao. Kwa kuwa huduma za malezi kupitia wadada hawa zinaweza zisikwepeke, ni muhimu kujadili namna gani tunaweza kupunguza uwezekano wa kumfanya msichana wa kazi akose ari na hamasa ya kufanya kazi yake kwa bidii. Makala haya yanajadili mapendekezo ya
namna ya kuboresha uhusiano na wadada wanaosaidia kazi na kulea watoto
majumbani. Fahamu
historia yake Ipo
haja ya kujitahidi kufahamu msichana ametoka familia gani, aliishi vipi na
familia yake, misimamo yake, imani, angalau mambo ya msingi. Ili hayo
yawezekane, ni vizuri kumpata kupitia watu wanaomfahamu vizuri. Unapokuwa
na fursa ya kumfahamu binti unayeishi naye vizuri, unaweza kufanya uamuzi
sahihi mapema ikiwa unaweza kukaa naye ama la. Mwelimishe
majukumu Mitafuruku
mingi kati ya waajiri na hawa mabinti wakati mwingine inachangiwa na
kutokufahamika kwa majukumu yake ipasavyo. Waajiri wengi huwa na matarajio
makubwa kwa akina dada na hivyo hawawasaidii kujua wanachopaswa kukifanya. Ni
vyema mara baada ya kukubaliana naye kuwa anaishi na familia yako kwa lengo la
kumwangalia mtoto, uhakikishe anajua utaratibu kamili wa kazi. Ukifanya hivyo
unapunguza uwezekano wa makosa yanayotokana na kutokujua jambo sahihi la
kufanya. Kujenga
uhusiano mzuri Mfanye
binti wa kazi awe sehemu ya familia yako. Mfanye ajisikie kupendwa kama
mwanafamilia mwingine. Unapofanya hivyo, unamfanya achangamke moyo na hivyo
kuwa na hamasa ya kujituma. Kwa
mfano, unaweza kumtambulisha kwa wageni kama sehemu ya familia yako na unaweza
kufikiria kumweka kwenye picha rasmi za familia unazoning’iniza ukutani. Sambamba
na hilo, epuka uhusiano usio wa kimaadili na wasichana hawa. Unapofanya hivyo,
unajenga mazingira ya kudharaulika. Ukidharaulika, ni rahisi mwanao kuwa
mhanga. Mpe
huduma anazostahili Hakuna
mfanyakazi ambaye hatamani kupata marupurupu. Hata wewe unahitaji mkubwa wako
wa kazi akuangalie kimaslahi, na atambue kazi nzuri unayomfanyia. Vivyo
hivyo, nawe fikiria kumpa msichana wako wa kazi huduma zinazomvutia.
Mtengenezee mazingira bora ya kazi. Kwa
mfano, unaweza kufikiria kumtengenezea utaratibu wa kujiendeleza kitaaluma. Pia
unaweza kuhakikisha unatambua kazi anazozifanya kila siku jioni unaporudi
nyumbani. Kwa kufanya hivyo unamjengea ari ya kazi. Onesha
mfano mzuri Huwezi
kutarajia binti wa kazi aishi vizuri na watoto, wakati wewe mwenyewe huoneshi
kuwajali. Onesha kwa vitendo namna unavyotarajia mtoto ahudumiwe. Binti
atajifunza kwa vitendo. Kadhalika,
kuwa mfano kwa kufanya kazi za ndani kama unavyotarajia afanye yeye. Pika,
tenga chakula mezani, fua nguo inapobidi ili kuonesha kuwa unaishi matarajio
yako. Unapofanya hivyo, binti atakuheshimu. Tumia
muda wa kutosha na mtoto Mtu
anayetumia muda mrefu na mwanao ndiye mwenye nafasi zaidi ya kuwekeza. Kwa
sababu binti ndiye anayekaa na mwanao kwa muda mrefu, upo uwezekano wa mwanao
kufundishwa mambo usiyoyatarajia. Ni
vizuri kuhakikisha unafuatilia maendeleo ya kitabia ya mwanao mara unaporudi
nyumbani. Jitahidi kuzungumza na mwanao kubaini ikiwa yapo yasiyofaa
aliyojifunza. Unapoyabaini, weka mbadala wake mapema. Pamoja na kuchukua hatua hizi, hatusemi kuwa mambo yatakuwa sawia. Zinaweza kuwapo changamoto, lakini si kama ambavyo hautajenga utamaduni wa kuwafatilia watoto. Christian Bwaya ni Mhadhiri wa Saikolojia, Chuo
Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU). Twitter: @bwaya, Simu: 0754 870 815. | 0 |
Patricia Kimelemeta SERIKALI imefuta diploma maalumu ya ualimu ambayo ilianzishwa kwa ajili ya kuongeza idadi ya walimu. Itakumbukwa wakati Serikali inaanzisha diploma hiyo, ilikuwa inakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu wa somo la sayansi. Diploma hiyo ilianzishwa na Serikali ya awamu ya nne, baada ya kujitokeza upungufu mkubwa kwa walimu wa masomo hayo na kutolewa kwenye vyuo mbalimbali, kikiwamo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Kwa mujibu wa waraka uliotolewa na Serikali na kusainiwa na Kaimu Kamishna wa Elimu Tanzania, Nicolas Burreta, ambao umeanza kutumika mwaka wa masomo 2016/17 katika vyuo vya elimu vya Serikali na binafsi, wizara ilihusisha programu za mafunzo ya ualimu mwaka 2014/15 ili kukidhi mahitaji ya sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014. Waraka huo, unasema hivi sasa wizara inaendelea na maandalizi ya sheria, kanuni na miongozo ya utekelezaji wa sera hii, ikiwamo uendeshaji na usimamizi wa mafunzo ya ualimu nchini. Sehemu ya waraka huo inasema: “Kwa kuzingatia maandalizi yanaendelea, mwongozo wa utekelezaji wa programu za mafunzo ya ualimu ya mwaka 2016/17 utakuwa wa mafunzo ya ualimu kwa astashahada (cheti) na stashahada. “Mafunzo hayo yataendeshwa kwa kutumia mtaala wa kitaifa ulioandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TEA) wa mwaka 2009 kwa astashahada na stashahada. Kutokana na hali hiyo, wizara itakuwa inatoa maelekezo ya sifa za kujiunga na mafunzo ya ualimu.” Pia unasema mafunzo hayo tarajali ya stashahada ya juu ya elimu ya sekondari yaliyokuwa yakitolewa kuanzia mwaka wa masomo 2014/15, yamehitimishwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte) na kutoa tuzo ya stashahada ya kawaida ya ualimu ya sekondari kwa wahitimu wa programu hiyo baada kukamilisha mwaka wa pili wa masomo. Aidha, wanachuo wanaoendelea na mafunzo tarajali ya ualimu wa stashahada ya kawaida kwa kutumia mtaala wa Tuzo za Taifa za Elimu ya Ufundi (NTA), wataendelea na mafunzo yao na kuhitimisha kama ilivyopangwa. “Programu ya mafunzo kazini ya stashahada ya elimu ya msingi iliyokuwa inatumia mtaala wa Tuzo za Taifa za Elimu ya Ufundi (NTA), imesitishwa ili kufanyiwa maboresho. “Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), litatahini na kutoa tuzo ya mafunzo ya ualimu ya astashahada na stashahada kuanzia mwaka wa masomo 2016/17 na kuvitaka vyuo vya ualimu kuhusika kutoa mafunzo ya ualimu (astashahada na stashahada) pekee, bila kuchanganya kozi nyingine. WADAU Akizungumza na MTANZANIA jana, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, alisema Serikali ya awamu ya nne iliamua kuanzisha programu hiyo kwa ajili ya kupunguza tatizo la upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi. Alisema kitendo cha Serikali ya awamu ya tano kuifuta, ni sawa kwa sababu wenyewe ndio waliamua kuanzisha na wenyewe ndio wameamua kuifuta, hivyo walimu wa masomo hayo watakwenda kutafutwa nje ya nchi. “Mpaka sasa kuna uhaba wa walimu wa sayansi, jambo ambalo limechangia Serikali ya awamu ya nne kuanzisha programu hii, kitendo cha kufuta ni uamuzi wao wenyewe, labda watakwenda nje ya nchi kutafuta walimu wa sayansi,” alisema Mukoba. Aliongeza vijana wengi waliosoma masomo ya sayansi na kuhitimu kidato cha sita wanakwenda chuo kikuu kutafuta taaluma nyingine, siyo ya ualimu, hivyo wananchi wategemee tatizo la uhaba wa walimu litaendelea siku hadi siku. “Kuna vijana wengi wanaohitimu kidato cha sita ambao wamesoma sayansi wanakwenda chuo kikuu kutafuta taaluma nyingine, ikiwamo ya udaktari na si ualimu, kwa mtindo huu tatizo la walimu litaongezeka,” alisema. Alisema Serikali imeamua kuboresha diploma ya msingi kwa walimu kwa madai ya kujipanga upya, lakini ni imani yao wakimaliza kujipanga watakuja na uamuzi mzuri ambao utasaidia kuboresha sekta ya elimu. Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC), Profesa Innocent Ngalinda, alisema uamuzi huo ni mzuri kwa sababu umelenga kuboresha sekta hiyo. Alisema siku hizi digrii ni sawa na elimu ya kidato cha nne, Serikali lazima ihamasishe walimu ili wajiendeleze. “Kuondolewa programu hii kutasaidia walimu wengi kujiendeleza kielimu, kwa sababu digrii ya sasa ni sawa na elimu ya kidato cha nne, tunapaswa kujifunza siku hadi siku ili twendane na wakati,” alisema Ngalinda. Alisema ili taifa liweze kupata maendeleo, linahitaji mwalimu bora ambaye amezalishwa katika chuo bora kwa ajili ya kutoa elimu bora zaidi. | 3 |
NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM NAHODHA wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amesema kuwa wamepania kupata ushindi dhidi ya Malawi ‘The Flames’ kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam keshokutwa ili kuondoa mdudu wa sare tangu Charles Mkwasa apewe kibarua cha kuinoa timu hiyo. Stars itamenyana na Flames katika mchezo wa awali wa kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi, Mkwasa ataingia kwenye mechi hiyo akiwa hajaambulia ushindi katika mechi mbili za mashindano alizoiongoza Stars, akiambulia sare mbili. Akizungumza na MTANZANIA jana, Cannavaro alisema sare dhidi ya Uganda na Nigeria zimetosha na sasa watahakikisha wanaanza kupata ushindi. “Hatuhitaji sare nyingine kwenye mchezo huu wa tatu tangu tuwe na kocha wetu Charles Mkwasa, hizo zinatosha na sasa ni ushindi tu tutahakikisha tunaanza na timu hii ili kujiwekea mazingira mazuri ugenini,” alisema. Nahodha huyo wa Yanga, alisema wachezaji wote wapo katika hali nzuri na wote nia yao ni moja ya kuhakikisha wanalipatia ushindi Taifa na kuongeza matumaini kwa mashabiki wa soka nchini na kuongeza mapenzi yao kwa timu hiyo. | 4 |
KUNDI la watalii 330 wakiwemo wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Jimbo la Zhejiang, China, wameahidi kuwa watakuwa mabalozi wazuri wa Tanzania na hifadhi zake kwa wenzao.Watalii hao ambao waliwasili nchini Mei 12, mwaka huu kwa ziara ya kitalii, waliondoka jana. Wakihojiwa na gazeti hili, walisema watawashawishi wenzao kuja kutembelea vivutio vya Tanzania.Akizungumza na gazeti hili, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi na Mawasiliano wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa), Paschal Shelutete alisema watalii hao walikuwa nchini kwa siku nne na wametembelea hifadhi kadhaa na kuahidi kuitangaza Tanzania mara warudipo kwao.Shelutete alisema walipokuwa nchini walitembelea hifadhi za Manyara, Serengeti na Ngorongoro na kuona vivutio vingi wakiwemo wanyama, na waliahidi watawashawishi wenzao mara warudipo ili nao waje kutembelea Tanzania.“Hilo lilikuwa kundi kubwa la kwanza kutembelea hifadhi zetu kutoka China, tunategemea watalii wengi zaidi kutoka nchi hiyo mara baada ya hao kurudi kwao, kwa sababu tumefungua masoko ya nchi za Asia na kundi hilo limeahidi kuitangaza vizuri Tanzania,” alisema Shelutete.Awali, watalii hao walipokelewa nchini Mei 12, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ambako katika kundi hilo walikuwemo wafanyabiashara na wawekezaji.Akizungumzia watalii hao, Shelutete alisema hilo ni kundi la kwanza miongoni mwa watalii 10,000 wanaotarajiwa kutembelea Tanzania katika kipindi cha miaka miwili hadi mitatu, chini ya mpango unaosimamiwa baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Bodi ya Utalii Tanzania na Kampuni ya TouchRoad International Holding Group ya China.“Tunaamini ndani ya ushirikiano huu, tutapokea watalii wengine kwenye hifadhi zetu kwa sababu hivi sasa tumeamua kufungua masoko mapya kwa kuiangalia Asia na hii inatokana na uchumu wao ni mzuri na sasa watabadili fikra za kwenda maeneo mengine ya utalii na kuamua kuja Tanzania kwa sababu wameshatambua vivutio tulivyo navyo,” alisema Shelutete.Mapema akiwakaribisha watalii hao, Waziri Mkuu alimshukuru Mwenyekiti wa Kampuni ya Touchroad Group, Liehui He kwa kuwaunganisha Watanzania na Wachina kupitia mpango wake wa kukuza utalii.“Mbali na kutuunganisha Watanzania na Wachina, tunashukuru pia kwa kuamua kuitangaza Tanzania kuwa nchi yenye fursa nyingi za kitalii duniani,” alisema Majaliwa.Waziri Mkuu aliwapongeza watendaji wa Bodi ya Utalii na kampuni za utalii kwa maandalizi na mapokezi mazuri kwa watalii hao.Pia alimpongeza Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kushirikiana na TouchRoad na kuifanya Tanzania ipokee watalii wengi.Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Palamagamba Kabudi alisema ujio wa watalii hao ni sehemu ya mpango mkubwa wa nchi wa kuongeza watalii kutoka China unaofahamika kama Tour Africa - The New Horizon.Hata hivyo, Shelutete alisema kundi la pili la watalii litawasili nchini muda wowote na kushauri taasisi na mamlaka za usafiri hususan Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL), kutumia fursa hizo kuboresha na kuanzisha safari za kwenda China moja kwa moja.Alisema iwapo kutaanzishwa safari za kwenye nchi hiyo na nchi nyingine za Asia moja kwa moja, kutasaidia kuteka soko la watalii, badala ya watalii hao kutumia mashirika mengine ya ndege yanayolazimika kupitia nchi nyingine kabla ya kuja Tanzania. | 3 |
BARAZA la Mawaziri nchini hapa limetangaza kuongeza mishahara kwa walimu wa shule za msingi na sekondari kwa asilimia 10 katika shule za serikali na binafsi kuanzia Machi mwaka huu.Hatua hiyo imefikiwa na kikao cha mawaziri kilichoongozwa na rais wa nchi hiyo, Paul Kagame. Walimu nchini humo wamefurahishwa na ongezeko hilo na kuwa yamefanyika baada ya maombi ya muda mrefu ya chama chao, hivyo kuamini kuwa mambo mazuri yanakuja. Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Rwanda (SNER), Faustin Harelimana, alisema hatua hiyo imeleta ahueni kwani wamekuwa wakiomba kwa muda mrefu.Kwa mujibu wa muundo wa malipo kwa walimu, malipo kwa walimu inategemea kiwango cha elimu pamoja na uzoefu. Novemba mwaka jana, seneta waliomba serikali kuboresha malipo kwa walimu ili yaendane na ukuaji wa uchumi. Walimu kwa miaka kadhaa wakitaka kiwango cha mshahara kufikia angalau Faranga 80,000 za nchi hiyo ili kuweza kukidhi mahitaji muhimu, kwani walimu wanaoajiriwa wakiwa na vyeti kwa shule za msingi wanalipwa faranga 44,000 ,wale wenye diploma Faranga 90,000, huku wenye shahada wakipokea Faranga 120,000. | 3 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.