text stringlengths 1k 17.3k | label int64 0 5 |
|---|---|
Stars ipo Rustenburg nchini Afrika Kusini kwa ajili ya michuano ya Baraza la Soka la Nchi za Kusini mwa Afrika, COSAFA ambayo wao na Ghana wamealikwa kutia ‘nakshi’.Na timu hiyo jana iliendelea na mazoezi yake kwa siku ya tatu tangu iwasili hapa, kwenye viwanja vya Michezo vya Rustenburg, katikati ya mji huu mdogo wa madini ya platinum.Nooij ambaye siku mbili zilizopita timu yake ilifanya mazoezi Uwanja Olimpia Park, ambako michuano ya Cosafa itafanyika, leo alikuwa akiwaelekeza wachezaji wake namna ya kusaka mabao.Alikuwa akiwaelekeza vijana wake namna ya kupanga shambulizi hadi kufika langoni kwa wapinzani na kufunga.Na katika mfumo huo, wachezaji wanne wote wa mbele walikuwa wanapishana nafasi, wakati mwingine wengine wakienda pembeni na kurudi katikati wakipishana.Unaonekana ni mfumo mzuri wa kusuka nafasi za mabao iwapo wachezaji watauelewa vizuri na kuufanyia kazi uwanjani. Ni mfumo ambao mipira inayowapita washambuliaji, viungo wanatakiwa kuifuatilia kumalizia kwa mashuti makali.Wote Mrisho Ngassa, John Bocco, Juma Luizo na Ibrahim Ajib walionesha umahiri wa kufunga na kupiga krosi. Viungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Mwinyi Kazimoto, Hassan Dilunga na Said Ndemla walikuwa makini katika kumalizia mipira inayowapita washambuliaji.Kocha Msaidizi, Salum Mayanga alikuwa katika lango lingine akiinoa safu ya ulinzi dhidi ya mashambulizi ya aina tofauti, hususan ya kutokea pembeni kutokana na mipira ya kona na krosi.Stars iliyopangwa Kundi A katika Cosafa, inatarajiwa kutupa kete yake ya kwanza Jumatatu Uwanja wa Olimpia dhidi ya Swaziland. Timu nyingine katika kundi hilo ni Lesotho na Madagascar, wakati Kundi B lina timu za Shelisheli, Namibia, Zimbabwe na Mauritius.Kila timu itakayoongoza kundi, itaungana na wenyeji Afrika Kusini, Botswana, Ghana, Malawi, Msumbiji na Zambia kwa ajili ya hatua ya robo fainali. | 4 |
['Kumekuwa na msisimko Kenya kufuatia taarifa kwamba Mohamed Salah mchezaji nyota wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, yupo nchini Kenya.', 'Kwa mujibu wa Gazeti la Standard, Mohamed Salah aliwasili Kenya jana Jumanne jioni na kuondoka leo Jumatano asubuhi mwendo wa saa moja.', 'Picha za mchezaji huyo zimechipuka katika mitandao ya kijamii hii leo zikimuonyesha akiwa katika mojawapo ya hoteli za kifahari mjini Nairobi.', '"Ndio. Salah alikuwa hapa. Aliwasili Jumanne jioni na kuondoka mapema leo asubuhi. Alikuwa katikati ya safari yake," afisa mmoja amenukuliwa na jarida la Game Yetu.', 'Wakenya katika mitandao ya kijamii hawakuweza kuizuia furaha yao kutokana na kusikia kuwa mchezaji huyo nyota yuypo nyumbani.', 'Baadhi wakichukua fursa kumkaribisha:', "Wengine wakitamani japo kumuona kama @hamooy_gacal, aliyeandika katika twitter na kuomba ujumbe wake usambazwe hadi umfikie mchezaji huyo nyota wa Liverpool, 'Nataka kukuona @MoSalah", " Nipo Nairobi, tafadhali nitafute'.", 'Swali ambalo baadhi wameishi kuuliza baada ya taarifa kuwa mchezaji huyo keshaondoka, ni kwanini kuingia na kuondoka ghafla?', 'Mshambuliaji huyo wa Misri na klabu ya Liverpool ndiye mchezaji bora wa mwaka wa shirikisho la Soka Barani Afrika kwa mwaka 2018 - ikiwa ni mara yake ya pili kushinda tuzo hiyo.', 'Salah, mwenye umri wa miaka 27, alimshinda mwenzake wa Liverpool Sadio Mane kutoka Senegal na mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang kuwani atuzo hiyo.', 'Salah pia alitawazwa Mwanakandanda Bora wa Mwaka wa Afrika wa BBC kwa mara ya pili mtawalia Desemba.', 'Aliwafungia Liverpool mabao 44 msimu wa 2017-18 na kuisaidia klabu hiyo kufika fainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ingawa walishindwa na Real Madrid.'] | 4 |
Mwandishi wetu SERIKALI ya Sweden imeipa Tanzania fedha za Sweden SEK. Bilioni 1.64 (Sh bilioni 435.79) kwa ajili ya msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu. Makubaliano ya msaada huo yamesainiwa jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini, Ulf Kallsting. James akizungumzia tukio hilo, alisema imesainiwa mikataba mitatu ya msaada huo ambayo ni, mkataba kwa ajili ya kusaidia bajeti ya Serikali wa Sh bilioni 159.59 kwa kipindi cha 2017/18 hadi 2019/2020, ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Sh bilioni 53.20 zitatolewa. Alisema fedha hizo zitaelekezwa katika kuboresha uhalisia wa bajeti ili kuweza kutimiza majukumu ya kisera, kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya kikodi na yasiyo ya kodi na kusaidia Serikali kutoa huduma nzuri kwa wananchi kupitia taratibu za manunuzi. Mkataba mwingine ni kwa ajili ya kusaidia Mpango wa Elimu kwa Matokeo (EPforR) wa Sh bilioni 235.40 kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2020/2021. “Baada ya ya Serikali kutimiza wajibu wake wa kupeleka fedha katika Sekta ya elimu kwa wakati, wameamua kutupatia fedha hizo ambazo Serikali tunazipangia kazi kulingana na vipaumbele”, alieleza James. Alisema Mpango wa Elimu kwa Matokeo ulianza mwaka 2015/2016 na katika kipindi hicho yamepatikana maendeleo katika ujenzi wa miundombinu ya madarasa, vyoo, mabweni. Utekelezaji wake umefanywa katika shule 361 kwenye Halmashauri 129 nchini. “Katika mpango huo vyuo 17 vya Walimu vimekarabatiwa ikiwa ni pamoja na kununua Kompyuta 260, magodoro 6,730 na viti 1,976,” alisema James. Mkataba wa tatu uliosainiwa ni wa Marekebisho ya Mkataba wa Mpango wa Kusoma, Kuhesabu na Kuandika wenye Dola za Marekani 94.8 zilizotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Global Partnership for Education (GEP) na kukabidhiwa kwa nchi ya Sweden ili iweze kuusimamia. Alisema Serikali ilisaini mkataba huo na Sweden Mei, 2015 na muda wa utoaji wa fedha hizo ulikwisha Agosti, 2016 na kubakia kiasi cha dola milioni 18.3 ambazo zitapatikana baada ya kusainiwa kwa mkataba huo. | 3 |
Na JANETH MUSHI-ARUSHA SPIKA wa Bunge Mstaafu, amewataka wakulima nchini kuachana na kilimo cha mazoea kinachotegemea ruzuku kutoka serikalini. Badala yake, amewataka wakulima hao kujiwekea akiba kwa ajili ya kununua pembejeo za kilimo. Kauli hiyo aliitoa juzi, alipokuwa akizungumza na wakulima katika Maonyesho ya Wakulima na Wafugaji ya Nanenane, Kanda ya Kaskazini, yanayoendelea katika viwanja vya Themi, jijini hapa. Makinda alisema kuwa, wakulima wengi wamekuwa wakitegemea ruzuku kutoka serikalini ambayo pia huwa haitoshi, jambo linalorudisha nyuma wakulima wengi na kushindwa kubadili maisha yao kupitia kilimo. “Pembejeo ni changamoto kwa wakulima, mimi siyo muumini sana wa ruzuku, ndiyo maana naona inatakiwa mkulima mwenyewe ajipange vizuri anapokuwa katika kilimo. “Lazima mkulima ajifikirie, kwamba amelima mwaka huu na amepata mazao fulani na alipolima mwaka jana alitumia mifuko mitatu ya mbolea na mapato aliyopata ayawekee akiba ya fedha za mifuko mitatu ya pembejeo kwa mwaka unaofuata. “Uzoefu wangu na ruzuku unaonyesha kwamba, unapofika wakati wa ruzuku ukipewa mfuko mmoja wa mbolea, hautakusaidia. “Lazima wakulima wajifunze kuweka akiba ili kuepuka tabia ya kugombea mfuko mmoja wa ruzuku, kwa sababu hiyo ni dalili ya kurudi nyuma kimaendeleo na inaleta umasikini zaidi badala ya kukupa maendeleo,” alisema Makinda. Alitaja changamoto nyingine inayowakabili wakulima kuwa ni pamoja na taasisi za fedha kushindwa kuwapa wakulima mikopo kwa wakati wanaoihitaji. Kuhusu mabadiliko ya tabianchi, kiongozi huyo alisema wakulima nchini wana wajibu wa kuwatumia wataalamu wa hali ya hewa ili wanapolima, wajue hali ya hewa kwa wakati husika itakuwaje. | 3 |
RAIS John Magufuli amewataka wateule wake kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na maslahi ya wanyonge na kuwa wavumilivu hata wanaposemwa vibaya.Rais Magufuli aliyasema hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akiwaapisha viongozi aliowateua juzi na kuwataka wakumbuke miiko na viapo walivyoapa na kwenda kutimiza wajibu wao.Walioapishwa jana ni Mathias Kabunduguru ambaye amekuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama Tanzania, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu, Godfrey Mweli, na Balozi Ally Sakila ambaye aliteuliwa hivi karibuni.“Mkumbuke viapo mlivyofanya hapa, natumaini mtaenda kutimiza wajibu wenu vizuri, mkumbuke miiko yenu na kuyatimiza kwa ajili ya wananchi,” alisema Rais Magufuli katika shughuli ambayo ilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na Jaji Mkuu, Profesa Hamis Juma.“Kazi za watu ni utume, mkawatumikie Watanzania kila mmoja kwa eneo lake, kazi zina changamoto kubwa, mkafanye kazi bila ya kumuonea mtu, Mungu awaongoze kwa kadri ya mioyo yenu,” alisema.Alisema kazi hizo ni lazima wawatumikie wananchi, na kwamba katika ziara yake mkoani Lindi, alikutana na malalamiko mengi ya watu wamedhulumiwa malipo yao ya korosho na ufuta tangu mwaka 2016 - 2017 hawajalipwa, na vyama vya ushirika 31 ndio vimedhulumu wananchi zaidi ya Sh bilioni 1.2.“Viongozi 99 wameshashikwa na mpaka juzi waliponipa taarifa milioni 255 zimerudishwa na nyingine zinaendelea kurudishwa, mnaweza kuona mtu kalima korosho yake kauza, kadhulumiwa, ameshakata tamaa unaweza kuona ni kwa namna gani dhuluma inatendeka kwa wananchi wanyonge,” alieleza Rais Magufuli.Alisema viongozi wana jukumu la kutetea wananchi na kufuta machozi yao, Sh milioni 255 kupatikana ni mwanzo mzuri, na kwamba amehakikishiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo kuwa fedha zote zitatemwa na waliochukua ili kusudi wananchi waliodhulumiwa warudishiwe.Akimzungumzia aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Hussein Katanga ambaye amemteua kuwa Balozi, alisema “Katanga nimemtoa ili akaniwakilishe nchi fulani vizuri. Umefanya kazi vizuri tangu ukiwa RAS (katibu Tawala wa Mkoa), mpaka ukawa Katibu Mkuu Tamisemi, mpaka Mtendaji Mkuu wa Mahakama, umefanya vizuri ndio maana nimekuchukua ukaniwakilishe vema katika nchi fulani.”Kuhusu Kabunduguru, alieleza, “Wewe ni mtaalamu wa reforms (mageuzi), umefanya mambo mengi Utumishi, na umetusaidia vizuri Tamisemi, naamini Mahakama utatusaidia vizuri, rekodi yako haina mashaka, bahati nzuri Mahakama inafanya vizuri chini ya Jaji Mkuu, Mahakama imekuwa kimbilio la wananchi.”Kwa upande wa Mweli, alisema, “Naibu Katibu Mkuu ulifanya vizuri Wizara ya Elimu, baadaye ukaenda Mambo ya Nje sasa naona utaweza kunisaidia Tamisemi upande wa Elimu, kasimamie kero zote za walimu, mashule, maabara, utendaji kama wenzako walivyosimamia vizuri nawe kasimamie.“Matumaini yangu utaangalia sana kero za walimu, promosheni zao, hakuna sababu ya walimu kulalamika, na watendaji wengine wa wizara, ukashirikiane na Jafo na makatibu wakuu wenzako mkayatimize vizuri.” | 3 |
WADAU wa elimu mkoani Kigoma wamevitaka vyombo vya ulinzi na usalama na vya sheria kuwachukulia hatua za kisheria wazazi na ndugu wanaoharibu ushahidi ili kufanya kesi za watu wanaowapa mimba wanafunzi na wanaofanya vitendo vya unyanyasaji kwa watoto wasihukumiwe.Walisema hayo kwa nyakati tofauti katika kikao cha Marafiki wa Elimu kilichoitishwa na shirika lisilo la Serikali la Maendeleo ya Wanawake Kigoma (KIWODE) kwa ufadhili wa Taasisi ya HakiElimu Tanzania.Walisema kuharibiwa ushahidi huo na unyanyasaji watoto kunachangia kufanya mamlaka kisheria kushindwa kuwaadhibu wakosaji. Mwalimu Mkulikila Gosbert wa Shule ya Sekondari Bitale katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na Mwalimu Yassin Nkala wa Shule ya Msingi Katwalo wilayani Kasulu, walisema kwa nyakati tofauti kuwa kitendo cha wazazi kuuharibu ushahidi au kuwaficha watuhumiwa ili wasiadhibiwe, kinarudisha nyuma mapambano ya kumaliza tatizo la mimba shuleni.Walimu hao walisema wamekuwa wakisimamia suala hilo kisheria, lakini vikwazo ni vingi kutoka kwa wazazi wanaopaswa kuwa walalamikaji. Akitoa taarifa ya utafiti uliofanywa na Marafiki wa Elimu kutoka KIWODE kuhusu hali ya mtoto wa kike katika kupata elimu, Katibu wa Mkoa wa Kigoma, Michael Mbago alisema mtoto wa kike anakabiliwa na changamoto kubwa zinazomfanya kutokuwa na uwiano sawa katika kuhudhuria masomo na mtoto wa kiume hata kama wanatoka familia moja. | 3 |
Bila shaka utakubaliana nami kuwa Diamond kamwe hakubali kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na mwanadada hivi hivi. Hili ni dhahiri kutokana wapenzi ambao amewahi kuwa nao, nani asiyemjua Wema, Zari, Hamisa na Tanasha je? Wote ni ufafanuzi kamili wa kilele cha urembo. Hawa wengine kando, licha kutangaza kuachana na wapenzi wake hawa wote, Diamond amewahi tu kumrudia mmoja na huyo ni Hamisa, hii ni baada ya mapenzi yao ya kichinichini kupenyeza na kuchangia kuivunja uhusiano wa msanii huyo na Zari. You Glow Differently When You're Actually Happy …🥰💅🏾 Dressed by – @mobettostyles A post shared by HamisaMobetto (@hamisamobetto) on Mar 13, 2020 at 4:05am PDT Diamond ameonekana kuegemea sana upande wa Mobetto licha ya mrembo huyo kutangaza kuwa hawezi kurudiana naye. Hivi majuzi katika mahojiano, Hamisa alieleza kuwa japo hawezi kurudiana na Mondi, anakiri kuwa msanii huyo amekuwa mzazi wa kuwajibikia kikamilifu swala la malezi kwa mwanawe. Urembo wa Mobetto unaweza kumtia mume yeyote majaribu na hivyo siko tyari kumlaumu Mondi. Hakuanza leo, Hamisa alikuwa mwanamtindo kwa muda, kutokana urembo wake wa kutisha akawa anarembesha video za wasanii kadhaa. Ebu niambie … ni mstari upi unaoupenda zaidi kwenye wimbo wangu mpya wa #Nipotezee …. kuangalia kazi yangu mpya Bonyeza Link kwa Bio yangu 👆🏽👄 A post shared by HamisaMobetto (@hamisamobetto) on Dec 21, 2019 at 3:23am PST Alipoonekana katika kibao wa Diamond, hakuna aliyejua kuwa walikuwa katika uhusiano wa kimapenzi. Nam, kando na urembo wake, Hamisa ni msiri, unakumbuka habari kuhusu uhusiano wake na Mondi ulipopenyeza? alieleza kuwa walikuwa katika uhusiano kwa miaka tisa. Hizi ni baadhi ya picha za Hamisa za kuthibitisha kuwa yeye ndiye malkia wa urembo Tanzania. Tweny tweny …. 🥂 . Blazer – @catwalk_connection 💕 A post shared by HamisaMobetto (@hamisamobetto) on Dec 30, 2019 at 9:25am PST ✨MZUKA✨ Ni nywele Mpya, ni nyepesi, yenye mawimbi mazuri kwa bei nafuu kabisa kutoka @PRIMAAFRO_HAIR ❤ MZUKA ✔Balozi @hamisamobetto ✔Nywele #MZUKA ✔Rangi #1/30T ✔Saloni @@touchofbeauty_tz ✔Picha @sakshed ✔️Make up – @makeupbyjojo #primaafro_hair #hamisamobetto A post shared by HamisaMobetto (@hamisamobetto) on Mar 10, 2020 at 2:52am PDT TUNASHONA 🧚🏾♀️ Karibu @mobettostyles boutique tukushonee . Kwa mahitaji ya kutengeneza Nguo za – Kitchen Party, :-Bridal Party :-SendOff :-Weddings :-Wedding Guest :-Bride Maids :-Maid of Honour :- Baby Shower :-Birthdays :-Red Carperts :-Graduations Na shughuli nyinginezo zote zinazohusisha kupendeza kimavazi…… Wasiliana nasi kupitia (Call/WhatsApp) No- 0677667788) Or follow us kwenye official page yetu ya instagram ya biashara @mobettostyles Tupo Kijitonyama Karibu na Shule ya Mama Salma Kikwete. Karibuni wote .❤️ A post shared by HamisaMobetto (@hamisamobetto) on Mar 9, 2020 at 7:43am PDT Money Day Dressed by – @mobettostyles 👌🏽 Hair – @certified_perucaz A post shared by HamisaMobetto (@hamisamobetto) on Mar 9, 2020 at 12:06am PDT | 1 |
Na RAMADHAN HASSAN -DODOMA MGANGA wa Tiba asilia, Ashura Mkasanga (33), anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma akituhumiwa kumuua Mariamu Saidi (17), mkazi wa Mkoa wa Kigoma kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili kisha kukichoma moto. Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, alisema mwili wa marehemu ulikutwa kwa mganga huyo katika Kitongoji cha Chang’ombe, Kijiji cha Chamwino Ikulu wilayani Chamwino. Alisema mwili huo ulikutwa ukiwa umekatwa shingo kwa kutenganishwa na kiwiliwili na kichwa kikiwa kimechomwa moto na kubaki fuvu lisiloweza kutambulika sura yake. Kamanda huyo alisema baadhi ya sehemu za mwili wa marehemu ambazo ni mkono wa kushoto, shingo, kifua na sehemu za siri ziliunguzwa kwa moto. “Mnamo tarehe 8 mwezi huu majira ya saa nne usiku katika Kitongoji cha Chang’ombe, Kijiji cha Chamwino Ikulu, mtu mmoja mwanamke aliyefahamika kwa jina la Mariamu Saidi (17), mkazi wa Kigoma aliuawa kwa kukatwa shingo yake,” alisema. Kamanda Mambosasa alisema mazingira ya tukio hilo yanaonyesha kuwa mganga huyo asiye na kibali cha kuendesha shughuli za tiba asili, analaza wagonjwa nyumbani kwake, kufanya matambiko na kupiga ramli chonganishi. Alisema wamewakamata watu 11 wakiwamo wasaidizi wa mganga huyo ambao ni Victor Daniel (24) na mume wa mganga huyo, Noel Mazengo (30). | 3 |
FOMU za kushiriki mbio za Ngorongoro Race 2019, ambazo zinatarajia kufanyika Aprili 20 zitaanza kutolewa Ijumaa mjini Karatu, imeelezwa.Mratibu wa mbio hizo, Meta Petro alisema juzi tayari baadhi ya wanariadha nyota wamethibitisha kushiriki mbio hizo za kilometa 21, akiwemo Alphonce Simbu ambaye hivi karibuni alifikia viwango vya kushiriki Michezo ya Olimpiki itakayofanyika Tokyo, Japan 2020. Simbu pia amefuzu kwa mashindano ya dunia ya riadha yatakayofanyika Doha, Qatar Septemba mwaka huu.Petro alisema kuwa mbali na wanariadha wa hapa nchini, pia wanariadha kibao kutoka Kenya wameonesha nia ya kushindana katika mbio hizo, ambazo mshindi wa kwanza anatarajia kuondoka na kitita cha Sh milioni 1. Alisema kuwa wameamua kuweka kituo kimoja cha usajili wa wanariadha ili kuhakikisha kila mwanariadha anayenunua fomu anapewa risiti na pesa stahiki inaingia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia mashine ya kielectoniki ya EFD.“Tutaanza usajili Ijumaa na kila mwanariadha atakayenunua fomu atapewa risiti ya TRA ili serikali ipate fedha zake stahiki kwa ajili ya maendeleo ya taifa, “alisema Petro, ambaye ni kocha wa timu ya taifa iliyoshiriki mbio za dunia za nyika Denmark Machi 30 mwaka huu. Alisema fomu ya wanaotaka kushiriki mbio za kilometa 21 zitatolewa kwa Sh 20,000 wakati zile za kilometa tano kila moja itauzwa kwa Sh 10,000 na kilometa 2.5, ambazo zitashirikisha watoto zitapatikana kwa Sh 5,000 kila moja.Alisema kuwa mbio hizo ambazo zitaanzia katika lango kuu la kuingilia na kutokea katika Hifadhi ya Ngorongoro, zinadhaminiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorogoro (NCAA) na zitamalizikia katika viwanja vya Mazingira Bora mjini Karatu, Arusha. Patro akitaja zawadi zingine alisema mshindi wa pili wa mbio za nusu marathon ataondoka na Sh 500,000 wakati mshindi watatu atapewa Sh 200,000, huku mshindi wa nne atapewa 100,000.Kwa upande wa kilometa 5, mshindi wa kwanza atapewa Sh 300,000 huku wa pili 200,000 wakati watatu atapewa Sh 100,000 huku zawadi zikiendelea kutolewa kuanzia mshindi wa nne hadi wa 10. Wakati huohuo, NCAA kupitia kwa Kaimu Meneja Mawasiliano wao Joyce Mgaya, washiriki 100 wa kwanza kumaliza mbio za kilometa 21 watapata ofa ya kutembelea hifadhi hiyo. | 4 |
Mwandishi Wetu -Singida BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 katika wilaya kadhaa nchini. Misaada iliyotolewa na benki hiyo inayoongoza kwa kutengeneza faida kati ya benki zote zinazofanya biashara humu nchini ndani ya miezi mitano mwaka huu, inahusisha vifaa vya ujenzi, madawati na vifaa vingine vinavyowezesha ukamilishaji wa miradi ya afya,elimu na usalama wa raia. Benki ya NMB imeshatoa msaada wa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa mikoa ya Kanda ya Kati. Akifafanua kuhusu misaada hiyo wakati akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani ingida, Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi, alibainisha kuwa misaada hiyo ya zaidi ya Sh milioni 200 iliyotolewa imelenga sekta ya elimu, afya na majanga kwa mikoa mitatu ya Kanda ya kati. Akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, MkoaniSingida, katika shule ya Sekondari ya New Kiomboi, Mlozi alisema fedha hizo zilizotolewa na NMB zimetumika kununua madawati, viti vya shule za sekondari,vitanda na vifaa tiba kwenye sekta ya afya. Aidha, alisema lengo la misaada hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali. Pia alisema misaada hiyo imekabidhiwa kwa baadhi ya shule, zahanati, hospitali katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Pia NMB walikabidhi madawati 250 na vitanda 80 vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 29.5 kwa baadhi ya shule za Wilaya ya Iramba mkoani humo. Katika hatua nyingine, Benki hiyo imevipatia kituo cha Polisi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro pamoja na shule ya msingi Msowelo mabati 160 yenye thamani ya Sh5 milioni kwa ajili ya kuezekea maboma. NMB iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni mpango wa kuzipunguza baadhi ya changamoto kwa taasisi za serikali hapa nchini, Meneja wa NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus, alisema na kubainisha kuwa msaada huo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ili kusaidia kuinua miradi ya maendeleo. Baraka alisema kuwa kati ya mabati hayo, kituo cha polisi wilaya kimepa tamabati 80 huku shule ya msingi Msowelo nayo ikipata mabati 80. | 5 |
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais- TAMISEMI zimedhamiria kuimarisha na kuyaongezea nguvu madawati ya malezi shuleni ili kuweza kuwaweka wanafunzi huru zaidi kutoa tarifa za vitendo vya ukatili wa kijinsia.Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Dk. John Jingu aliyasema hayo jijini Dar es Salaam leo Alhamisi katika mdahalo wa kitaifa kuhusu ndoa za utotoni na ukeketaji ulioandaliwa na wizara hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), pamoja na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA).“Tayari walimu wa malezi wapo katika shule zote, lakini tutakachofanya ni kuyaimarisha madawati hayo ili yaweze kusimamia na kushughulikia masuala haya ya ukatili wa kijinsia, tunaamini wanafunzi wakipewa elimu ya kutosha wanaweza kutoa taarifa za kina endapo watafanyiwa au watashuhudia vitendo vya ukatili” alisema.Alisema, serikali inafanya jitihada mbalimbali kuhakikisha wanabadilisha fikra hasi ili kuhakikisha mtoto analindwa na katika kukabiliana na ukatili sambamba na kupambana na ndoa na mimba za utotoni zipo sheria mbalimbali zimewekwa ili kuhakikisha wanamlinda mtoto kwa vitendo.Alisema chanzo cha ukatili kwa watoto ni pamoja na mila potofu, fikra na imani za watu, umaskini na tamaa ya mali na kwamba serikali imejiwekea mikakati mbalimbali ua kukabiliana na jambo hilo.“Tunachopaswa kujiuliza ni kwanini tunafanya vitendo hivi? Tunathamini utamaduni wetu ila kuna tamaduni nyingine zinaleta maumivu na ni ukatili kwa jamii zetu na hivyo kuathiri mambo mengi ikiwemo mfumo wa elimu na kuendeleza umaskini” alisema.Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Dodoma, Fatma Toufiq alisema mkoa wao ni miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa ndoa za utotoni lakini wameanzisha kauli mbiu ya 'magauni manne kwa mtoto wa kike', ikiwemo sare ya shule, joho la kumaliza shule, gauni la harusi na gauni analovaa mjamzito.Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima alisema ukatili wa wanawake na watoto umejificha chini ya mila, desturi na tamaduni na kusema kwamba ushirikiano unahitajika kumaliza tatizo hilo kwa kuwa hakuna mwanamke anayependa kupigwa wala mtoto anayependa kuolewa bila kusoma.Naye Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Kivulini, Yassin Ally aliwataka wazazi na walezi kutoa mahitaji kwa watoto wao ili wasishawishike kwa kuwa wamebaini kwamba wengi wanaojiingiza kwenye mapenzi katika umri mdogo wengine wanashawishiwa na fedha kulingana na mahitaji yao. | 3 |
Tanasha Donna alitua Kenya pamoja na mwanawe Machi 24 baada ya kubainika kuwa uhusiano wake na msanii Diamond Platnumz uliingia mchanga. Hii ni siku chache tu baada ya Tanasha mwenyewe kuyakana madai kuwa uhusiano wao ulikuwa unakumbwa na matatizo na kusistiza kuwa uhusiano wake na Mondi u imara na wala hautikiswi. Tofauti zao zilianza kuwa bayana pale Mondi alipoamua kuitoroka hafla yake ya kipekee ya uzinduzi wa kanda ya mpenziwe huyu nchini Kenya akidai kuwa alikuwa na suala la dharura humu Tanzania. Tofauti kati ya Diamond na mpenziwe imeibua hisia kali mitandaini wengi wakimlaumu Tanasha kwa kujiingiza katika uhusiano huo kama kipofu licha ya kuona jinsi msanii huyu alivyowatema wapenziwe wa awali. Sasa yupo shabiki mmoja ambaye ameamua kumpigia goti mamake Dangote akitaka aingilie kati na kuwapatanisha Mondi na Tanasha. Mama dinyooooo.. site 🏡 A post shared by Sandrah…! (@mama_dangote) on Mar 9, 2020 at 1:07am PDT Ikimbukwe kuwa uhusiano wa Mondi na Tanasha ulipoanza, mamake Mondi alikuwa katika mstari wa mbele akimsifia mrembo huyo na hata kumshauri mwanawe kufunga naye pingu za maisha rasmi. Lakini baada ya uhusiano huo kusambaratika, fununu zimetokea zikidai kuwa mama Mondi ni kati ya walioandaa hafla kusherehekea kusambaratika kwa uhusiano huo. Swali ni je, mama Dangote ana uwezo wa kumshawishi mwanawe akamkubali Donna tena, na je, iwapo Mondi atakubali kurudiana na Donna, je Donna mwenyewe atakubali. Isisahaulike kuwa muda mfupi baada ya kubainika kuwa Donna na Mondi walitofautiana, Donna alijitokeza wazi na kusimulia jinsi Mondi alivyokuwa akimtumia vibaya. Nam, licha shabiki huyo kuwaomba wawili hao kurudiana, wapo wengi waliojitokeza na kumkashifu na kumshambulia Donna wakimshauri kutorea kabisa kwao Kenya na kuanza shughuli ya kumlea mwanawe pasi kumhusisha Mondi. Kutokana na picha ambazo Dona amekuwa akipakia mitandaoni baada ya kuachana na Mondi, ni bayana hajuti kwa hatua aliyoichukua. Picha hizo zote zinamuonyesha akifurahia maisha yake akiwa huru. | 1 |
MIAMBA ya soka nchini, Simba na Yanga leo itakuwa kwenye viwanja viwili tofauti kuendelea na kampeni za kulisaka taji la Ligi Kuu Bara.Mechi hizo zitachezwa saa nane mchana ambapo vinara wa ligi hiyo, Yanga watakuwa uwanja wa Jamhuri Morogoro kumenyana na Mtibwa Sugar na mabingwa watetezi, Simba watakuwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga kumenyana na wenyeji wao Coastal Union. Yanga inaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kushinda mchezo wao wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa kwa mabao 2-1 katika mzunguko wa kwanza.Kocha mkuu, Mwinyi Zahera aliitumia jana asubuhi kuendesha mazoezi kwa wachezaji wake katika uwanja wa Jamhuri tayari kwa mechi hiyo. Yanga leo itawakosa wachezaji wake nyota wawili ambao ni beki kisiki, Kelvin Yondani mwenye kadi nyekundu na Feisal Salum mwenye kadi tatu za njano. Pamoja na kukosekana kwa wachezaji hao, kocha mkuu huyo amejawa na matumaini kibao ya kupata ushindi wa mchezo huo baada ya kurejea kwa nahodha wa timu hiyo Ibrahim Ajibu na Abdallah Shaibu ‘Ninja’.Kwa upande wa timu ya Mtibwa Sugar ambayo ni mwenyeji wa mchezo huo na yenye pointi 45 na kushika nafasi ya tano ya msimamo wa Ligi Kuu, itaingia uwanjani chini ya Kocha mkuu Zuberi Katwila, kwa kuhitaji kuvuna pointi tatu muhimu. Kwa upande wa mabingwa watetezi Simba wanaingia kwenye uwanja wa Mkwakwani kwa nguvu zote baada ya kung’olewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ilipoweka rekodi ya kucheza robo fainali msimu huu.Kutokana na ushiriki wake kwenye michuano ya kimataifa, Simba ina viporo tisa, ikiwemo cha Coastal. Simba inatakiwa kumaliza viporo hivyo ili kulingana na washindani wake kwenye taji Yanga na Azam waliokwishacheza michezo 31 kila mmoja. Hasira za wekundu hao ni kushinda michezo yao hiyo ili kutetea taji la ubingwa. Timu hiyo kwa sasa ina pointi 57 baada ya kucheza michezo 22.Kocha wa Simba, Patrick Aussems alisema anaiheshimu Coastal Union kama ilivyo kwa TP Mazembe iliyowaondoa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mabao 4-1 na wamefika mkoani hapo (Tanga) wakiwa na malengo ya kupata pointi tatu muhimu.“Tunamheshimu Coastal kama mwingine yeyote, tunahitaji kutetea ubingwa wetu kwa hiyo tumekuja kupambana,” alisema na kuongeza kuwa anajivunia kuwa walishinda mechi 10 mfululizo zilizopita, hivyo anatarajia kuongeza mchezo wa 11 na wachezaji wake wanaweza.Kocha wa Coastal, Juma Mgunda alisema: “ni mechi itakayokuwa na ushindani mkubwa kwasababu sote tuna malengo, Simba inataka kutetea taji nasi kukaa sehemu nzuri kwenye ligi. “Naamini itakuwa ni mechi yenye ushindani lakini sisi tumejiandaa vizuri. Vijana wako vizuri, tuko tayari kupambana kupata pointi tatu,” alisema. | 4 |
NA SOSTSHENES NYONI-DAR ES SALAAM HAKUNA ubishi, Suleiman Matola ana heshima kubwa katika Klabu ya Simba yenye maskani yake Mtaa wa Msimbazi, jijini Dar es Salaam. Heshima aliyonayo Matola Simba inatokana na jinsi alivyojitoa kwa moto kuitumikia klabu hiyo nyakati zake akiichezea, ambapo alipata kuwa kiungo hodari na kuisaidia kutwaa mataji. Hili lilisababisha uongozi wa Simba kumpa heshima ya kuwa nahodha wa kikosi chao. Ikumbukwe pia ubora wa Matola uliishawishi klabu ya Super Sport ya nchini Afrika Kusini kumsajili kutoka Simba. Hata hivyo, Matola, ambaye baada ya kustaafu soka aliamua kugeukia ukocha na kuzifundisha klabu kadhaa, ikiwamo ya sasa ya Lipuli inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, sasa ana sura nyingine tofauti na anapotazamwa na mashabiki na wapenzi wa klabu ya Simba. Tangu alipokabidhiwa jukumu la kuinoa Lipuli msimu uliopita kutoka mikononi mwa raia wa Uganda, Richard Amatre, timu hiyo imekuwa kikwazo kikubwa kwa Simba kuvuna pointi tatu. Rekodi zinaonyesha Lipuli tangu iliporejea Ligi Kuu msimu uliopita na kuwa chini ya Matola, haijawahi kupoteza mchezo dhidi ya Simba, mbali ya kumalizika kwa sare. Hili ndio linalowafanya mashabiki na wapenzi wa Simba wasahau kwa muda mazuri yote aliyowahi kuyafanya Matoka akiwa mchezaji wa timu yao na kumtazama kama mwanajumuiya aliyewaasi. Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, matokeo yalikuwa sare ya bao 1-1. Katika mchezo huo, Simba ilifunga bao la kuongoza kupitia kwa kiungo James Kotei, lakini beki Asante Kwasi aliizawazishia Lipuli kwa mkwaju wa mpira wa adhabu. Timu hizo zilipokutana katika mchezo wa mzunguko wa pili kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa, matokeo yalikuwa sare ya bao 1-1. Lipuli ilitangulia kuandika bao kupitia kwa Adam Salamba, kabla ya Simba kusawazisha dakika za majeruhi kupitia kwa aliyekuwa mshambuliaji wao raia wa Burundi, Laudit Mavugo. Ni katika mchezo huo, kiwango cha juu cha Salamba kiliwavutia mabosi wa Simba ambao waliamua kumsajili katika kikosi chao anachokitumikia msimu huu wa Ligi Kuu. Matola na Lipuli yake imeendelea kuonekana kuwa mlima mrefu kwa Simba hata msimu huu wa Ligi Kuu. Hilo lilidhihirika katika mchezo wa kati ya timu hizo uliopigwa juzi Uwanja wa Taifa, ambako dakika 90 zilimalizika kwa suluhu. Huo ulikuwa mwendeleo wa sare timu hizo zinapokutana katika michezo ya Ligi Kuu. Hatujui nini kitatokea timu hizo zitakapokutana katika mchezo wa mzunguko wa pili mkoani Iringa, ni suala la kusubiri na kuona.
Akizungumzia sare ya juzi dhidi ya Simba, Matola anakiri kwamba, wapinzani wao ni timu imara, hivyo alipaswa kuisoma kwa kina ili kuhakikisha hapotezi mchezo na kama akilazimika basi iwe sare. “Simba wanatumia viungo wengi sana, kwa mantiki hiyo, ili uweze kuwamudu unatakiwa na wewe kujaza viungo wa kutosha katikati. “Baada ya kuwasoma niliingia na plani hiyo na kweli ilitusaidia, unaweza kuona licha ya kwamba hatukupata ushindi, lakini tuliwamudu na kutengeneza nafasi za kutosha, ingawa hatukuzitumia,” alisema Matola na kuongeza: “Njia pekee ya kuimudu Simba ni kujaza viungo wa kutosha, kinyume na hapo utawapa nafasi ya kutawala mchezo na mwisho itakugharimu.” Matokeo ya juzi kati ya timu hizo yaliifanya Simba ishindwe kumfikia na hata kumporomosha mpinzani wake Yanga, ambayo Ijumaa iliyopita iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mwadui FC na kukwea nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu, ikifikisha pointi 29. Simba baada ya sare ya Lipuli, imesalia nafasi ya tatu, ikiwa na pointi 27, Azam ndio vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 33. | 4 |
WAHITIMU 7,122 wanatarajiwa kutunukiwa vyeti katika mahafali ya tisa ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), hivyo kufanya idadi ya wahitimu katika chuo hicho tangu kuanza kwake kufikia zaidi ya 43,000.Aidha, mahafali hayo pia yatatumika kumuaga Mkuu wa Chuo hicho, Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ambaye Machi mwakani atakuwa anamaliza kipindi chake cha kuongoza chuo hicho.Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Peter Msoffe ambaye alikuwa akizungumzia mahafali hayo yatakayofanyika kwa siku mbili kuanzia kesho katika ukumbi wa Chimwaga.Alisema kati ya wahitimu hao 69 ni wa cheti, 673 wa Stashahada, 6,125 ni Shahada ya kwanza, 16 wa Stashahada za juu, 220 ni Shahada za Uzamili na 19 wa Shahada za Uzamivu.“Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Benjamin William Mkapa atahudhuria mahafali hayo ya siku mbili ambayo pia yatahudhuriwa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Gaudentia Kabaka,” alisema.Alisema katika siku ya kesho, yatakuwa ni mahafali ya ndaki tano za Elimu, Sayansi za Ardhi, Afya, Sayansi za Kompyuta, Habari na Mawasiliano na Sayansi Asilia na Hisabati.Profesa Msoffe alisema mahafali ya siku ya Ijumaa yatakuwa ya ndaki mbili za Sanaa, Lugha na Sayansi za Jamii na ile Taaluma za Biashara na Sheria. Aidha, Profesa Msoffe alisema mahafali hayo yatatanguliwa na Mkutano Mkuu wa Jumuiko la wahitimu unaofanyika leo, ambapo mtoa mada mkuu atakuwa Balozi wa India nchini, Sandeep Arya ambaye atawasilisha mada juu ya Maisha ya Mahatma Gandhi na mchango wake kwa jamii.Akizungumzia kumuaga, Kaimu Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Msoffe alisema kwa mujibu wa Hati Idhini ya chuo Mkuu wa Chuo, Rais mstaafu Mkapa anamaliza muda ikiwa ameshatumikia vipindi viwili.Akizungumzia mipango ya maendeleo, Profesa Msoffe alisema mpango wa kujenga ndaki zilizobaki, upo kwenye hatua za kutafuta gharama na michoro. Profesa Msoffe alisema kwa upande wa shule ya sekondari, ambayo inafadhiliwa na serikali kwa asilimia 100 iko kwenye ujenzi. Alisisitiza kuendelea na mpango wa upandaji miti katika kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.Akizungumzia mafanikio, Profesa Msoffe alisema hospitali ya chuo imepanda hadhi kutoka Kituo cha Afya hadi Hospitali ya Wilaya, hivyo chuo kina mpango wa kujenga majengo mengine zaidi ili kuweza kupanua uwezo wa utoaji wa huduma. Aidha, alisema Chuo na Hospitali ya Benjamini Mkapa wakishirikiana na Madaktari bingwa kutoka Tokushukai Medical Corporation na Tokyo Women’s Medical University ya Japan, wamefanikiwa kupandikiza figo kwa wagonjwa watatu. | 3 |
ASKARI wa kikosi cha barabarani wameagizwa kutekeleza agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola la kupiga marufuku upigaji wa tochi nyuma ya gari na kuzirusha.Aidha, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amefafanua makosa yenye dhamana na ambayo watuhumiwa hawapaswi kukaa mahabusu zaidi ya saa 24.Masauni amesema hayo akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) aliyelalamikia upigaji tochi magari kwa nyuma na kusema umeendelea kufanyika.Selasini amesema licha ya Waziri Lugola kutoa maelekezo kwa askari kutopiga gari tochi kwa nyuma, mtindo huo unaendelea miongoni mwa askari. Aliomba Masauni kufafanua suala hilo.Akijibu kuhusu kesi ambazo mtuhumiwa anapaswa kuwekwa ndani chini ya saa 24, Masauni alisema makosa yote isipokuwa yaliyoanishwa katika kifungu 148 (5) (a) hadi (e) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 yana dhamana na watuhumiwa hawapaswi kukaa mahabusu zaidi ya saa hizo.Swali hilo ni la Mbunge wa Shaurimoyo, Mattar Ali Salum (CCM).Amesema watuhumiwa wanaokaa ndani saa 24 ilhali makosa yao yana dhamana, hutokana na sababu za kushindwa kutimiza masharti na vigezo vya dhamana.Vigezo hivyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kifungu cha 65 na 66 Sura ya 20 ilivyorekebishwa mwaka 2002. | 3 |
Mechi ya leo inatarajiwa kuwa ya vuta nikuvute kutokana na timu hizo kufanya vizuri kwenye mechi zao zilizopita mpaka kufika fainali.Azam inacheza fainali kwa mara ya pili tangu ilipofanya hivyo mwaka 2012 michuano hiyo inayoshirikisha mabingwa wa nchi za Afrika Mashariki na Kati ilipofanyika nchini na kufungwa mabao 2-0 na Yanga.Azam, mshindi wa pili wa ligi ya msimu wa mwaka 2014/2015 ilipata nafasi ya kucheza fainali baada ya kuifunga KCCA ya Uganda bao 1-0 wakati Gor Mahia ilifuzu hatua hiyo kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Al Khartoum ya Sudan.Utamu wa mechi ya leo unasubiriwa kwa hamu kwani timu zote zimekuwa zikicheza kandanda safi na lenye kuvutia.Akizungumzia mechi hiyo kocha wa Azam, Stewart Hall alisema anatarajia kupata matokeo mazuri katika mchezo huo wa leo.“Kama nilivyosema tangu mashindano haya yanaanza kwamba lengo letu lilikuwa ni kufika fainali, na sasa tuko kwenye fainali, na kazi iliyo mbele yetu ni kutwaa ubingwa, jambo ninaloamini kuwa litatimia,” alisema.Alisema anafahamu ugumu wa mechi hiyo kwa vile wapinzani wao pia wazuri lakini hata wao ni wazuri, hivyo timu nzuri zimekutana. “Timu nzuri na bora zimeingia fainali, natarajia kuona mechi ngumu kesho (leo) na mshindi atakuwa mshindi kweli,” alisema.Alisema anawaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi kushuhudia mechi hiyo, kwani sasa imekuwa si ya Azam peke yao, ila ni ya taifa lote.“Azam tunawakilisha nchi, wenzetu wengine walishatoka (Yanga na KMKM) kwa hiyo Watanzania waje kutuunga mkono tunawategemea sana, tunawaahidi ushindi,” alisema.Kwa upande wa kocha wa Gor Mahia, Frank Nuttal amesema anatarajia kukutana na ugumu kwenye mechi hiyo kwa vile timu wanayokutana nayo ni nzuri, lakini pia inacheza nyumbani.“Wanasema timu ikiwa nyumbani ina nafasi kubwa ya kushinda hivyo tutacheza kwa tahadhari, kwani tunajua Azam licha ya kwamba ni timu nzuri lakini ina nafasi kubwa sababu iko nyumbani… “Na sisi tumejipanga, hatuidharau Azam tunaiheshimu kwa maana ni timu nzuri na inajua kutafuta ushindi,” alisema.Wakati Azam FC inasaka rekodi ya kutwaa kwa mara ya kwanza taji hilo iliyolikosa mwaka 2012, wenzao Gor Mahia watakuwa wakisaka kulitwaa taji hilo kwa mara ya nne baada ya kulibeba 1980, 1981 na 1985, huku Simba ikiwa ndiyo bingwa wa kihistoria baada ya kulitwaa taji hilo mara sita mwaka 1974, 1991, 1992, 1995, 1996 na 2002. | 4 |
KOCHA Msaidizi wa timu ya soka ya Malindi, Ahmed Saleh Machupa amesema matokeo ya sare waliyoyapata wakiwa ugenini sio mabaya na wanajipanga kuhakikisha wanashinda katika mechi yao ya nyumbani.Malindi ambayo inashiriki Kombe la Shirikisho barani Afrika ilishuka uwanjani katika dimba la Amaan kucheza na Mogadishu City ya Somalia ambao walikuwa ugenini baada ya wapinzani wao hao kuomba kuutumia kutokana na kwao Somalia kutokuwa na usalama.Machupa amesema mchezo huo pamoja na kuwa ulichezwa katika uwanja wake wa nyumbani, lakini kiuhalisia wao ni wageni na wachezaji wake walicheza kwa umakini mkubwa kwa kuhofia kufungwa.Hivyo alisema kuwa katika mchezo unaofuata, ambao Malindi watakuwa nyumbani, wamepania kushinda ili kusonga mbele hatua inayofuata.Aidha alisema kuwa kupitia mchezo wao wa juzi wamebaini udhaifu kwao na kwa wapinzani wao, hivyo wataufanyia kazi kabla ya kurudiana wiki mbili zijazo.“Wapinzani wetu udhaifu wao tumeuona na sisi tumeonesha udhaifu wetu, lakini tunaondoka hapa na kwenda kuyafanyia marekebisho,” alisema.Kwa upande wake kocha wa Mogadishu City, Mohammed Mistri Lamjed amesema kuwa walicheza kwa tahadhari sana ili kuhakikisha hawapotezi mchezo huo.Alisema mechi hiyo kwao ilikuwa ngumu sana kutokana na kwamba walicheza wakiwa ugenini ingawa walikuwa wao ni wenyeji wa mchezo huo.Katika mchezo wao wa awali miamba hiyo ilifanikiwa kutoka na sare isiyokuwa na mabao ambapo kila mmoja anahitaji ushindi wa angalau kuanzia bao 1-0 ili iweze kusonga mbele. | 4 |
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Fatuma Latu amesema baada ya miaka miwili au mitatu Bagamoyo itakuwa tofauti na kama ndoto zake zikitimia za kutekekeleza miradi mikubwa watu wengi watavutiwa kuwekeza huko.Amesema, anatamani kuacha alama kwa kulibadilisha eneo hilo kupitia miradi mikubwa ukiwemo ujenzi wa stendi ya kisasa, kuendeleza fukwe, kujenga soko la kisasa la samaki, kuwa na meli kubwa za uvuvi na kupata mwekezaji mkubwa kwenye bandari.Latu amesema ofisini kwake kuwa, ametumia fursa ya kuandika maandiko kwa ajili ya miradi mkakati na anatamani ndoto zake zitimie.“Kwa hiyo mimi kwa kweli napambana sana kupata hii miradi, kama nikipata kwa mfano nimeshaandika, nimesimamia hapa na kuratibu mradi wa soko la samaki ambalo tunategemea kwa sasa hivi ule mkataba tumeupeleka kule kwa Mwanasheria Mkuu aufanyie vetting hopefully wiki ijayo yaani natamani yule mkandarasi aanze kufanya kazi pale kujenga soko kubwa la samaki la kisasa”amesema.Ameyasema hayo wakati akizungumza na timu ya wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani 2019 na Kongamano la Fursa za Biashara na Uwekezaji mkoani humo.“Lakini natamani twende mbali zaidi, baada ya soko tungetamani kuvutia watu wawekeze kwenye meli kubwa za uvuvi. Tunayo bahari, tunayo access, kama soko litakuwepo la kisasa, lina refregaration, lina miundombinju mizuri kwa nini wasije wavuvi wakubwa kama ambavyo wanafanya kule Mwanza”amesema.Kwa mujibu wa Latu, soko la samaki Bagamoyo litakuwa na maeneo mbalimbali likiwemo la kupaa, kuhifadhi, kuuzia na maegesho kwa ajili ya wateja wanaokwenda kununua.“Kwa hiyo naamini kwa kuboresha hilo litaacha legacy (kumbukumbu), lakini pia kama nilivyosema hutuna land bank, na maeneo mengi yalipangwa lakini hayakufidiwa kwa hiyo ni magumu kwenda kuanza uwekezaji kwa hiyo tulitafuta eneo la stendi, Bagamoyo haina stendi kubwa” amesema.Amesema, kwa sababu ya kasi ya uchumi wa viwanda, suala la usafirishaji litakuwa muhimu kwa Bagamoyo hivyo wamekubaliana na mwananchi ambaye atatoa ekari 16 ijengwe stendi ya kisasa inayotarajiwa kuwa na huduma mbalimbali yakiwemo maduka makubwa, na maegesho ya malori na magari mengine.Kwa mujibu wa kiongozi huyo mchumi, eneo hilo tayari lina hati na amewasilisha andiko hazina kwa ajili ya kupata fedha.“Kwa hiyo tunaamini nitaacha structure kubwa ambayo itakuwa ni kumbukumbu kwangu”amesema.Amesema kwa muda mrefu wamekuwa na kiu ya kuwekeza eneo la ufukwe la BADECO (Bagamoyo Development Corporation) lakini wamekuwa wakishindwa kwa sababu ya tatizo la umiliki. | 5 |
WAZIRI wa Kilimo, Dk Charles Tizeba amezitaka kampuni za uwindaji wa kitalii nchini kuongeza michango ya fedha na huduma kwa jamii inayozunguka mapori ya akiba nchini.Akizungumza na watendaji wa Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin Conservation Fund(FCF) inayomiliki kampuni za uwindaji wa kitalii, katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoani Simiyu, Dk Tizeba amesema kuna kampuni zinapata fedha nyingi lakini uchangiaji jamii ni ndogo."Nyie najua mnafanya vizuri lakini wenzenu katika maeneo mengine hadi wamefikia hatua ya kuwachagulia miradi wananchi," amesema.Ofisa Uhusiano wa FCF, Clarence Msafiri amesema kampuni zilizo chini ya taasisi hiyo zimekuwa zikitoa kwa jamii asilimia 20 ya mapato yao kila mwaka.Alisema kampuni zao ikiwepo Mwiba Holding na TGTS na walizowekeza wilayani Meatu pori la Akiba la Maswa na Makao, licha ya kutoa michango ya kijamii pia kwa mwaka wanatoa kwa vijiji zaidi ya Sh milioni 610 kama kodi ya pango.Meneja ujirani Mwema wa kampuni ya Mwiba Holdings, Alfred Mwakivike alisema kampuni hiyo kabla ya kusaidia miradi imekuwa ikipata maelekezo ya halmashauri.Alisema miradi wanayoitekeleza ina thamani zaidi ya Sh bilioni mbili na yote imeidhinishwa na Halmashauri ya Meatu.Taasisi ya Friedkin inashiriki Maonesho ya Nanenane kwa mara ya kwanza kuhamasisha uhifadhi, kupiga vita ujangili na pia kuonesha umuhimu wa uhusiano wa uhifadhi na kilimo. | 5 |
UTAFITI uliofanyika katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam umeonesha kuwa wilaya hiyo imekumbwa na uhaba mkubwa wa kondomu.Katika taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kudhibiti Ukimwi kwa kipindi cha robo tatu Januari hadi Machi, mwaka huu, inaonesha kuwa kondomu zimeadimika katika wilaya hiyo, kitu kinachochea ongezeko kubwa la maambukizi ya virusi ya Ukimwi.Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti Ukimwi, Manispaa ya Kinondoni, George Manyama alisema kondomu zimeadimika baada ya wafadhili wa masuala ya Ukimwi kujitoa akitolea mfano Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), kitu ambacho kimefanya kondomu kuwa adimu katika vituo vya afya, madukani na hata nyumba za kulala wageni. “Baraza la Madiwani lishauri serikali iondoe kodi katika uingizaji wa kondomu, ili upatikanaji wake uwe rahisi, na ziweze kusambazwa kwa wingi katika maeneo hatarishi,” alisema.Alisema kondomu zilizoadimika ni zile za Sh 500, Sh 1,000 na za Sh 5,000 kitu ambacho ni hatarishi kwani kitachochea ongezeko la maambukizi ya Ukimwi kwa wingi ndani ya wilaya hiyo. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Faustine Ndugulile, akizungumzia hilo alisema wana taarifa juu ya suala hilo la kuadimika kwa kondomu maeneo mbalimbali nchini na kwamba hatua za haraka zimeanza kuchukuliwa.“Changamoto imetokea, baada ya kubadilisha mfumo uliokuwapo kwa wale wasambazaji wa taasisi binafsi, jukumu hilo limerudi ndani ya wizara, hivyo kuanzia sasa ndiyo itakuwa inasimamia manunuzi, usambazaji wa mipira ya kiume. “Utaratibu uliokuwapo (awali) kulikuwa na baadhi ya taasisi ambazo zilikuwa zinapewa fedha na kununua mipira kisha kuisambaza kwa bei nafuu, ndiyo maana zilikuwa zinapewa majina mbalimbali kupitia hizo taasisi.“Utaratibu wetu serikali tutakuwa tunanunua mipira hiyo na kuigawa kwenye vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya na kwenye jamii. “Hivyo tumelibaini hilo tatizo katika kipindi hiki cha mpito, kwa kushirikiana na wenzetu tutahakikisha tuna kondomu za kutosha ndani ya wiki moja, kuanzia sasa zitakuwa zimeanza kupatikana,” alisema. Hata hivyo, taarifa hiyo ya uhaba wa kondomu Wilaya ya Kinondoni imekuja siku chache baada ya tafiti kutolewa kuwa asilimia 24 ya wanaume wilayani humo wana tatizo la nguvu za kiume. | 3 |
Na SHARIFA MMASI-DAR ES SALAAM MCHEZAJI wa gofu kutoka Arusha, Nuru Molel, juzi ameibuka bingwa katika mashindano ya gofu ya Kombe la Waitara, kipengele cha wachezaji wa kulipwa (Professionals) ambayo yalifanyika viwanja vya Lugalo, jijini Dar es Salaam. Molel aliwashinda jumla ya wachezaji wa kimataifa 21 walioshiriki michuano hiyo, kwa gloss 71, huku nafasi ya pili ikimwendea John Loence pia wa Arusha, aliyeshinda kwa gloss 72. Hassan Kabio wa Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam alimaliza nafasi ya tatu baada ya kushinda kwa gloss 72, ambapo washindi walitarajiwa kukabidhiwa zawadi zao jana jioni. Waitara Trophy iliendelea jana kwa kushirikisha vipengele vyingine, isipokuwa watoto wenye umri chini ya miaka 18. “Hakutakuwepo na ushiriki wa watoto wenye umri chini ya miaka 18 kutokana na mashindano haya kudhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti,” alinukuliwa nahodha wa Klabu ya Gofu ya Lugalo, Japhet Masai. Waitara Trophy hufanyika kila mwaka, lengo ni kukumbuka mchango wa mwanzilishi wa Uwanja wa Gofu Lugalo, Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jenerali Mstaafu George Waitara. | 4 |
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetahadharisha wananchi hususani wafanyabiashara nchini kote kuchukua tahadhari kuhusiana na wimbi la matapeli wanaojifanya maofi sa wa mamlaka hiyo.Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam siku za hivi karibuni kuna matapeli ambao wamekuwa wakipigia watu simu na kujifanya maofisa wa TRA na kwenda kwa wafanyabiashara na kuwatisha kwa lengo la kujipatia fedha. “TRA ina utaratibu wake rasmi wa kuwasiliana na wafanyabiashara na kuwajulisha siku rasmi ambazo maofisa watakwenda kufanya ukaguzi na unafanyika kwa uwazi bila vitisho,” alisema.Alisema tangu Desemba mwaka jana wamekuwa wakipata malalamiko kutoka kwa watu tofauti tofauti ambao wamekuwa wakitapeliwa fedha na maofisa TRA hao feki na kwa sasa wameona suala linaota mizizi na wasipochukua hatua kwa haraka itaharibu jina la TRA na sifa za maofisa wa mamlaka hiyo.“Kama mtu atapigiwa simu au kama una mtu una wasiwasi naye tafadhali toa taarifa kwa ofisi zetu zilizopo karibu nawe au toa taarifa kituo cha huduma kwa wateja namba 0800780078 au 08800750075 kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa moja usiku na utupe namba ya mhusika ili tuweze kufuatilia. “Pia kuna namba ya WhatsApp 0744233333 ambayo unaweza kutoa taarifa au kuuliza chochote saa 24.Ni maalumu kutatua changamoto za wananchi na kuwawezesha kulipa kodi kwa wakati,” alisema. Kayombo aliwataka wananchi kulipa kodi ya majengo kwa wakati badala ya kusubiri tarehe rasmi ya malipo hayo kuepusha usumbufu. Alisema viwango vipya vya kodi vilivyopitishwa na Bunge mapema mwaka huu vya kodi vya majengo ya kawaida sasa ni Sh 10,000 kwa majengo ya mijini na vijijini.Marekebisho hayo yaliwasilishwa chini ya Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbali Mbali Namba 2 wa Mwaka 2019, Februari 9, 2019 na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi.Alisema serikali ilipendekeza Sheria ya Serikali za Mitaa ya utozaji wa Kodi ya Majengo, lengo likiwa ni kiwango mfuto vya kodi ya majengo na kuiwezesha TRA kuwa mkusanyaji pekee wa kodi ya majengo. Alisema viwango vingine vya kodi ya majengo vilivyopitishwa na Bunge ni Sh 20,000 kwa nyumba za ghorofa maeneo ya vijijini na Sh 50,000 kila sakafu kwa nyumba za ghorofa katika maeneo ya mjini. | 3 |
Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima Kanda ya Kati(TASO) Shabaan Myombo wakati wa uzinduzi wa maonesho ya mifugo kitaifa na ya Nanenane Kanda ya Kati uliofanyika katika Uwanja wa Nzuguni mjini hapa.“Wakulima wengi sasa wanatumia matrekta madogo ya kusukumwa na mkono, matrekta madogo na hata makubwa, matrekta zaidi ya 1,000 yaliyokuwepo tayari yamenunuliwa na wakulima na sasa zaidi ya wakulima 800 wamejiandikisha ili kupata mkopo wa matrekta,” alisema.Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mahmood Mgimwa alisema kaulimbiu ya mwaka huu ya ‘Matokeo Makubwa Sasa, kilimo na mifugo ni biashara’ ina lengo la kuamsha ari kwa wakulima na wafugaji ili kuongeza tija na kufanya shughuli za kilimo na mifugo kuwa za kibiashara.Alisema hilo litawezekana kwa kupitia matumizi ya zana bora za kilimo, wanyama kazi na utumiaji wa matrekta madogo ya kusukumwa na mkono.Alisema katika kupunguza changamoto za masoko, mikoa ya Kanda ya Kati ihamasishe utekelezaji wa dhana ya kilimo cha mkataba ili wakulima wa mikoa ya Kanda ya Kati wawe na soko la uhakika la mazao wanayozalisha kwa kuzingatia vigezo vya ubora vitakavyowekwa na wanunuzi wa mazao hayo. | 5 |
ZAINAB IDDY -DAR ES SALAAM WIKI iliyopita kocha wa timu ya Taifa
ya Tanzania, Taifa Stars, Emmanuel Amunike, alitaja kikosi cha awali cha
wachezaji 39, kwa ajili ya maandalizi ya fainali za Afrika (Afcon), zitakazofanyika
nchini Misri kuanzia Juni 21 hadi Julai 19. Mbali ya fainali hizo, kikosi hicho
kitajiandaa na mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Misri, utakaochezwa Juni
13, mwaka huu Uwanja wa Borg El Arab, jijini Alexandria. Akizungumzia wakati akitangaza kikosi hicho, Amunike, alisema pia amelenga kuwaandaa wachezaji aliowaita kwa ajili ya fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (Chan). Afcon, Stars imepangwa Kundi C
pamoja na jirani zao Kenya, Algeria na Senegal, wakati Misri ambao ni wenyeji
wapo Kundi A pamoja na Zimbabwe, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
(DRC). Kundi B linaundwa na Burundi, Madagascar, Guinea na Nigeria. Kundi D lina Namibia, Afrika Kusini,
Ivory Coast na Morocco, wakati Kundi E, imo Angola, Mauritania, Mali na Tunisia
huku Kundi F likiwa na Guinea Bessau, Benin, Ghana na mabingwa watetezi,
Cameroon. Ikumbukwe Taifa Stars imefuzu Afcon baada ya kumaliza nafasi ya pili kwenye Kundi L na kukusanya pointi zake nane, nyuma ya Uganda iliyoongoza kwa pointi 13, Lesotho iliyomaliza nafasi ya tatu na pointi sita na Cape Verde iliyokamata nafasi nne na pointi tano. Tanzania itashiriki Afcon kwa mara ya pili tu katika historia, baada ya mwaka 1980 ilipofanyika nchini Nigeria ambako ilipangwa Kundi A pamoja na wenyeji Nigeria, Misri na Ivory Coast na kushika mkia. Katika michuano ya mwaka 1980, Taifa Stars ilifungwa mechi mbili, kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Nigeria na kichapo cha mabao 2-1 ilichokipata kwa Misri kabla ya kutoa sare ya 1-1 na Ivory Coast na kuishia raundi ya kwanza, michuano hiyo ilishirikisha timu nane. Kwa upande wa Chan, Taifa Stars
itaanzia nyumbani dhidi ya Sudan Julai 26 kabla ya kurudiana Agosti 2 na
ikifuzu mtihani huo itamenyana na mshindi kati ya Kenya na Burundi. Walioitwa kwa Afcon Makipa: Aishi Manula (Simba SC),
Metacha Mnata (Mbao FC), Suleiman Salula (Malindi SC) na Aaron Lulambo
(Tanzania Prisons), wakati kwa upande wa mabeki wapo, Claryo Boniface (U20),
Hassan Kessu (Nkana FC, Zambia), Vincent Philipo (Mbao FC) na Shomari Kapombe
(Simba). Wengine ni Mohammed Hussein
‘Tshabalala’, Erasto Nyoni (Simba SC), Kelvin Yondani, Gardiel Michael (Yanga
SC), Abdi Banda (Baroka FC, Afrika Kusini), Ally Mtoni (Lipuli FC), David
Mwantika, Aggrey Morris (Azam FC), Ally Ally (KMC) na Kennedy Wilson (Singida
United). Viungo wapo Feisal Salum, Ibrahim Ajibu (Yanga SC), Himid Mao (Petrojet, Misri), Frank Domayo, Mudathir Yahya (Azam FC), Jonas Mkude (Simba SC), Shiza Kichuya (ENNPI, Misri), Simon Msuva (Difaa Hassan El-Jadidi Morocco), Farid Mussa (Tenerife, Hispania) na Freddy Tangalu (Lipuli FC). Washambuliaji wapo Yahya Zayd (Ismailia, Misri), Shaaban Iddi Chilunda (Tenerife, Hispania), Rashid Mandawa (BDF, Botswana), Ayoub Lyanga (Coastal Union), Kassim Khamis (Kagera Sugar), Miraj Athumani (Lipuli FC), Kelvin John (Serengeti Boys), Adi Yussuf (Solihull Moors, England), John Bocco (Simba SC), Thomas Ulimwengu (JS Saoura, ALgeria) na Nahodha Mbwana Samatta (KRC Genk, Ubelgiji). Makocha, wachambuzi wa soka wametoa maoni yao baada ya kikosi cha Taifa Stars kutangazwa. Kennedy Mwaisabula ambaye ni kocha na mchambuzi wa soka nchini anasifu uteuzi lakini anasema kikosi hicho kinahitaji muda wa kutosha wa kukaa pamoja kabla ya kwenda kwenye mashindano. “Kikosi hakijabadilika sana na kile cha siku zote kinachoonekana hapa wachezaji wengi wameitwa baada ya kelele zilizokuwa zikipigwa na watu mbalimbali. “Kuna wachezaji hawakustahili kuwepo
katika kikosi na huenda wameitwa kwa kuwa watu wengi walihitaji wawepo, lakini
kwa kuwa kocha ndiye mtu wa mwisho na mwenye maamuzi hatuna budi kumpa
ushirikiano kwa manufaa ya Tanzania,” anasema. Kwa upande wa Ally Mayay ambaye ni
mchezaji wa zamani wa Taifa Stars na mchambuzi anasema: “Kikosi kilichoitwa ni kizuri kwa kuwa ndicho kilichotuwezesha
kufika Afcon. “Hivi sasa Stars inahitaji mechi
nyingi za kirafiki ili kujiweka kiushindani tofauti na hapo tunaweza kuwa
washiriki tu na si washindani.” Amunike anenaKocha Amunike anasema anahitaji mechi mbili ngumu kwa ajili ya kukiandaa kikosi chake kuelekea kwenye michuano ya Afcon. “Nahitaji michezo miwili migumu kwa ajili ya kuandaa kikosi kuelekea kwenye michuano ya Afcon ambayo tumeweza kufuzu, tupo tayari kupambana na kupata matokeo ila ni lazima tupate mechi mbili.” | 4 |
Na Waandishi Wetu RAIS Dk. John Magufuli, amewakosoa baadhi ya watendaji wa Serikali waliombeza aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, wakati wa sakata la kashfa ya Escrow. Rais Magufuli alisema Kafulila ameonesha uzalendo mkubwa ambao hauwezi kusahaulika katika historia ya Tanzania na kumpongeza kwa hatua yake ya kujitoa muhanga kutetea rasilimali za Watanzania. Akizungumza na wananchi wa Kata ya Nguruka jana katika uzinduzi wa mradi mkubwa wa maji uliopo Tarafa ya Nguruka katika Wilaya ya Uvinza alisema atakuwa mnafiki akishindwa kumpongeza Kafulila kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuibua ubadhirifu uliofanywa na Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL. Alisema Kafulila alitukanwa sana alipo ibua sakata la Escrow na kuitwa majina mengi ya kudhalilishwa kama tumbili na mengine mengi ya ajabu kwa sababu ya uzalendo wake wa kutetea Taifa. “Mimi ninafahamu unapoibua kitu cha kizalendo lazima usemwe, hivyo ninampongeza Kafulila kwa uzalendo wake kwa nchi na nitaendelea kumpongeza maisha yangu yote” alisema. Rais Magufuli alisema maendeleo hayana chama ndio maana Kafulila alijitoa kwa hali ya juu na kutetea fedha za umma zilizo kuwa zikiibwa na mafisadi wachache na kujinufaisha wao wenyewe. “Ninajua Kafulila ulitukanwa sana wakati wa kuibua sakata la Escrow, wapo watu walikuita tumbili mimi najua wewe sio tumbili, wao ndiyo matumbili. “Kafulila wewe hongera alisimamia wizi tuliokuwa tunafanyiziwa IPTL. Ni wizi wa ajabu na wengine wakamtisha kumpeleka mahakamani, wakamtukana weee! Na wengine wakamwita tumbili, sasa tumbili amefanya kazi kubwa kwa ajili ya Watanzania. “Tunahitaji wazalendo katika nchi hii, nchi hii ilikosa uzalendo ikawa na watu watafutaji, ukimchagua kiongozi anatafuta pesa yake badala ya kwenda kuongoza kwa ajili ya watu ambao ni masikini. “Tulikosa uzalendo wa utanzania, tukashindwa kumwogopa Mungu kwamba mali ni za muda tu baadae tutaziacha na kwenda kwenye shimo moja tu (kaburini) tutakapozikwa kule kaburini. Ninawaomba Watanzania tujenge uzalendo. “Kafulila wewe najua ni wa chama kingine, lakini umefanya kazi kubwa ya kulinda maslahi ya nchi, kwa hiyo nitakuwa mnafiki sana nisipo kupongeza. Kitu ulichokifanya kwa taifa ni kikubwa naomba nikupongeze kwa hilo,” alisema. Alisema kiongozi mzuri ni yule ambae anatetea wananchi bila kujali chama wala siasa za uchochezi, hivyo atahakikisha kuwa wananchi hawateseki na wale ambao wameiba fedha za Serikali wanazirudisha bila kujali nyadhifa walizonazo ili pesa hizo zitumike katika kuleta maendeleo. Rais Magufuli aliwaahidi wananchi wa Nguruka kuwa atahakikisha anatatua kero ya maji na umeme katika kata yao, wakati katika suala la umeme atamtuma Waziri wa Nishati na Madini ili aweze kutatua tatizo hilo na kuwasaidia. Rais Magufuli amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku tatu Mkoani Kigoma kwa kuweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa maji katika Kata ya Nguruka uliogharimu zaidi ya Sh bilioni 2, ambao unatarajiwa kukamilika Desemba 30 mwaka huu. Kafulila Akizungumza na MTANZANIA jana, Kafulila ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini kupitia (NCCR- Mageuzi), alimshukuru Rais Magufuli kwa kutambua kazi aliyokuwa akiifanya na sasa imeanza kuleta matokeo mazuri. “Kwa kweli nafarijika na inanipa moyo wa kizalendo zaidi ninapoona Rais anaunga mkono sakata la Escrow ambalo mimi ndo nililiibua wakati nikiwa mbunge japo nilipitia kwenye kipindi kigumu. “Nimefarijika sana mkuu wa nchi kuguswa na kutambua mchango wangu katika vita hatari ya ufisadi wa IPTL / ESCROW, natambua kwenye vita hii hakuna chama. “Niliteseka sana ndani na nje ya jimbo kutokana na vita hii, zilifanyika kila hila na njama lakini Namshukuru Mungu kuwa upande wangu hata nimebaki hai,’’alieleza Kafulila. Aliendelea kueleza. “Ukweli nimefarijika sana kuona mkuu wa nchi amelizungumzia jambo hili jimboni kwa wananchi walionipenda sana amezungumzia kwa hisia na uzito wa kutosha binafsi kwenye vita ya ufisadi nchini ninamuunga mkono Rais ,”alieleza Kafulila. Kafulila alimshauri Rais ajenge mfumo wa taasisi imara za uchunguzi na uendeshaji wa mashtaka katika eneo hilo ili kuhakikisha vita hiyo inakuwa ya mafanikio makubwa. Msuguano Kafulila alipoibua sakata hilo alipata upinzani mkubwa ndani na nje ya Bunge, ambapo kulikuwa na mvutano mkali kati yake na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, wanasiasa na watendaji wengine wa Serikali waliohusishwa na sakata hilo. Wakati Bunge likiwa linaendelea mwaka 2014 katika hali isiyokuwa ya kawaida kuliibuka na mvutano mkali baada ya Kafulila kuomba mwongozo juu ya ESCROW na wizi uliofanyika. Werema wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alipotakiwa kutoa maelezo, kwanza alianza kushambulia vielelezo vya Kafulila kuwa ni vipeperushi visivyokuwa na maana hali hiyo ilipelekea Mbunge wa Ubungo wakati huo, John Mnyika (Chadema) kudai kuhusu utaratibu lakini mwenyekiti wakati huo Mussa Zungu alipotezea. AG aliendelea kumtaka Kafulila wakutane nje kama anamambo mengine ila bungeni kunautaratibu wake (walikuwa wakimwingilia wakati anazungumza wakionesha kutokubaliana naye). Majibishano yalipozidi Werema alipandwa na hasira alisema. “Kafulila wewe ni sawa na tumbili asiyeweza kuamua mambo ya msituni,” alisema na baadae Kafulila aliposimama naye alimwita Werema mwizi. Kutokana na mvutano huo Werema alionesha dalili za kutaka kumfuata Kafulila akampige, lakini baadhi ya mawaziri walimzuia na kumsihi atulize hasira.
Baada ya Bunge kuahirishwa wakiwa nje Jaji Werema alilalamika hadharani kuhusu Kafulila kumwita mwizi ndani ya Bunge na ndipo jaji huyo alipotaka kumvamia tena Kafulila. “Mimi nakwambia Kafulila nitakukata kichwa, we subiri tu labda ukiniomba msamaha” alisema Werema kwa sauti ya hasira. Kutokana na maneno hayo Kafulila naye alijibu. “Huwezi kunikata kichwa, huwezi, yaani uniue, hapana huwezi tena nakwambia huwezi,” alisema Kafulila. Ampongeza Sakaya Wakati huo huo akiwa mkoani Tabora, Rais Dk. Magufuli amempongeza Mbunge wa Jimbo la Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF), kwa kazi nzuri anayoifanya katika kuwaletea wananchi maendeleo licha ya kuwa anatoka chama cha upinzani. Dk. Magufuli alitoa kauli hiyo jana wilayani Kaliua mkoani Tabora alipokua akizindua barabara ya Kaliua-Kazilabwa yenye urefu wa kilomita 56 iliyojengwa kwa kiwango cha lami na Kampuni ya Chico ya China. Dk. Magufuli alisema kuwa ni heri kuwa na mbunge wa upinzani anayetekeleza mambo ya Chama Cha Mapinduzi kuliko kuwa na mbunge wa CCM anayetekeleza ya upinzani kwani huo ni usaliti mkubwa kwa chama. “Nasema haya kwa sababu nafahamu hata wakati wa kampeni niliyashudia haya, ndiyo maana nasema ni bora kuwa na mbunge wa CUF, Chadema anayetekeleza mambo ya CCM kuliko wa CCM anayetekeleza mambo ya vyama vingine. “Najua mwili wake wote na akili yake yote ni CUF lakini damu yake ni CCM” alisema Dk. Magufuli. Akizunguzia ujenzi wa barabara hiyo Dk. Magufuli alisema imejengwa kwa fedha za Serikali bila mfadhili kuchangia, ambapo aliwataka wananchi kutozidisha uzito wa mizigo na kuchimba mchangan kado ya barabara ili idumu kwa muda mrefu. Aliutaka Wakala wa Barabara (Tanroads) kubomoa nyumba zote zitakazojengwa katika hifadhi ya barabara bila kutoa taarifa. “Kuna zoezi litaanza hivi karibuni la kubomoa nyumba ziliopo kando ya reli, hakikisheni zote zinaondoka, tunaaza kujenga reli ya kisasa lazima nyumba zote ziondoke kupisha ujenzi, najua wapo viongozi wengine wa CCM wanapitishapitisha maneno wa kubomoa anzeni na za hao wa CCM” alisema Dk, Magufuli. Ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 56 umegharimu zaidi ya sh bilioni 61.9 ambazo ni pamoja na gharama za ujenzi, usimamizi na fidia kwa wananchi waliopisha utekelezaji wa mradi huo. Wakati huo huo Dk. Magufuli amemwagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, kutangaza zabuni ya ujenzi wa barabara ya Kaliua hadi Urambo yenye urefu wa kilomita 28 kwa kiwango cha lami ndani ya mwezi mmoja kutoka sasa. “Tafuteni mkandarasi kama hamjampata ndani ya mwezi mmoja apatikane msaini mkataba, pesa zipo hata mkitaka kesho njooni mchukue” alisema. Akizungumzia kero zinazowakabili wakulima wa tumbaku Dk. Magufuli alisema suala hilo amemwachia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alishughulikie na kisha kumpelekea taarifa. Alizitaka mamlaka husika kutotumia nguvu kubwa kuwaondoa waliovamia misitu badala yake wawaeleweshwe ili watafahamu madhara ya uharibifu wa mazingira. Kuhusu suala la mimba shuleni, Rais Magufuli aliwataka wanaume wanaowapatia wanafunzi ujauzito kujiandaa kwenda jela miaka 30 ili wakatumie nguvu zao kuzalisha wakiwa gerezani. Habari hii imeandaliwa na Editha Karlo, Kigoma, Leonard Mang’oha na Asha Bani, Dar Mwisho | 3 |
Hadi dakika ya 30 Yanga ilikuwa inaongoza kwa mabao mawili. Maboa hayo yamefungwa na Papii Tshishimbi kwa penati na Obrey Chirwa.Mabingwa hao watetezi ni wa pili kwenye msimamo wa ligi kuu Tanzania bara wakiwa na pointi 34 na wanahitaji ushindi ili kuwakaribia vinara Simba, ambao wanaongoza wakiwa na pinti 41.Simba kesho watashuka dimbani kucheza na Mwadui FC kwenye Uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga, Majimaji inayofundishwa na Habib Kondo, jana ilifanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kocha huyo akisema kuwa mchezo huo utakuwa na ushindani.“Najua mchezo utakuwa na ushindani kwasababu Yanga itahitaji kushinda kama sisi ambavyo tunahitaji kushinda ili kutoka katika mstari wa timu zinazofanya vibaya,” alisema Habibu Pia Kondo alisema, wachezaji wake wamejiandaa vya kutosha na wana ari ya mchezo na wamemwakikishia kuondoka na pointi tatu.Yanga yenye pointi 34 endapo itashinda bado itaendelea kubaki katika nafasi ya pili, kwani wapinzani wao Azam FC juzi walicheza na kutoka sare na kubaki nafasi ya tatu.Azam ilitoka sare na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba na kufikisha pointi 34 sawa na Yanga lakini wwakitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa. Majimaji ina pointi 14 katika nafasi ya 14 ikiwa na pointi sawa na Kagera Sugar na Mji Njombe, ambazo zipo kwenye nafasi za mwisho.Vinara Simba ambayo itakuwa wageni wa Mwadui FC kwenye Uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga kesho endapo itashinda itaendelea kuweka pengo la pointi saba na mahasimu wake Yanga. | 4 |
PATRICIA KIMELEMETA NA LEONARD MANG’OH -DAR ES SALAAM JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limefanya upekuzi nyumbani kwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu kwa saa 5, baada ya kumshikilia tangu juzi. Lissu, alikamatwa juzi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakati alipokuwa akitoka kwenye kesi ya mwanachama wa chama hicho, Yericko Nyerere, ambayo ni wakili. Baada ya kukamatwa, alifikishwa Kituo Kikuu cha Kati, Dar es Salaam na kuandikiwa makosa mawili ambayo ni kumkashifu Rais Dk. John Magufuli na uchochezi kuhusu kushikiliwa ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 nchini Canada. Kutokana na hali hiyo, polisi walikwenda nyumbani kwa Lissu jana asubuhi kufanya upekuzi na walipomaliza walimrudisha kituoni saa 7:53 mchana. MKONDYA Alipotafutwa Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar as Salaam, Lucas Mkondya ili kuzungumzia suala hilo, alithibitisha kuendelea kumshikilia Lissu. Alisema hadi jana, walikuwa wanaendelea na upelelezi kuhusu makosa yanayomkabili. “Tunamshikilia Lissu tangu juzi. Baada ya kumkamata, askari walikwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi, walipomaliza wamemrudisha kituoni,” alisema Mkondya. Alisema anashangazwa na kitendo cha waandishi kufuatilia suala moja la Lissu wakati kuna matatizo mengi kwa wananchi, lakini hayaripotiwi. “Laiti muda mnaotumia kufuatilia suala la Lissu mngekuwa mnafuatilia matatizo ya jamii, tungejua mambo mengi ambayo tungeweza kuyashughulikia kuliko kuhangaika na suala moja la Lissu,” alisema. Hata hivyo, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, alisema polisi walienda nyumbani kwa Lissu kwa upekuzi na walipomaliza walimrudisha Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa taratibu nyingine za kisheria. Alisema kutokana na hali hiyo wanasubiri kama kiongozi huyo atapewa dhamana au la kwa sababu sheria iko wazi kuhusu hilo. Agosti 20, mwaka huu, Lissu alisema ndege ya tatu aina ya Bombardier Q 400 iliyotarajiwa kuwasili nchini mwishoni mwa Juni, mwaka huu, imekamatwa nchini Canada kwa amri ya mahakama kutokana na deni la Dola za Marekani milioni 38.7 (Sh bilioni 87) ambazo Serikali inadawa na mkandarasi iliyemvunjia mkataba wake wa ujenzi mwaka 2009. Alisema amri hiyo ilitolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC), baada ya mkandarasi huyo, Stirling Civil Engineers Ltd kufungua shauri akiishtaki Serikali ya Tanzania kwa kuvunja mkataba wake wa ujenzi wa barabara kutoka Wazo Hill hadi Bagamoyo. Alisema kutokana na hali hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Agustine Mahiga na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Jack Zoka, walikutana na mdeni huyo ambaye alikubali kuachia ndege hiyo endapo yatafanyika malipo ya awali ya Dola milioni 12.5. | 3 |
SAKATA la basi la Spider lenye namba za usajili KBQ 907J kukamatwa na Tume ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) likidaiwa kuwa na kemikali bashirifu zinazotumika kutengeneza dawa za kulevya, limechukua sura mpya baada ya tume kusema bado inawasaka wahusika zaidi wa suala hilo.Katika mahojiano maalum na gazeti hili jana, Kamishina wa Tume ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Kamishna William Sianga na Kamishna wake wa Operesheni, Frederick Milanzi walisema bado tume inachunguza tukio hilo ili kuwakamata wahusika wanaotuhumiwa.Basi hilo lilikamatwa Septemba 10, mwaka jana likitoka Jiji la Nairobi nchini Kenya kwenda jijini Dar es Salaam na linashikiliwa hadi leo. Hadi sasa zaidi ya mwaka mmoja, tume hiyo inamshikilia kondakta wa basi hilo, Jumanne akidaiwa kuhusika na usafirishaji mzigo huo.Chanzo cha habari kililieleza gazeti hili mmoja wa wamiliki wa mabasi ya Spider alikamatwa baada ya tukio hilo lakini alitoroka baada ya kuwekewa dhamana na hajulikana alipo hadi sasa huku kukiwa na taarifa ya kutokamatwa kwa mtu aliyemwekea dhamana hadi sasa.Kamishna Sianga alisema jana Tume yake bado inalifanyia kazi suala hilo ili kuwapata wahusika wote waliohusika na ununuzi na usafirishaji wa mzigo huo suala linalofanyiwa kazi na Milanzi.Milanzi alisema kipindi chote hicho mtu pekee anayeshikiliwa nao ni kondakta wa basi hilo. Alisema kushikiliwa kwa kondakta kunatokana na kuwa msimamizi wa basi ambaye kitaratibu ndiye anayehusika na mizigo iliyo ndani ya basi.Alisema hata hivyo, kondakta huyo si mtu pekee anayehusika na sakata hilo bali bado Tume inafanya uchunguzi wa kuwabaini wahusika wote ili kuwafikisha katika vyombo vya sheria.“Bado tunawatafuta wahusika kujua ni akina nani. Hadi sasa hatujaweza kumtambua na kwa sababu hakuna mtu ambaye tuna taarifa zake za kuhusika na mzigo huo, tunalifuatilia,” alisema. | 3 |
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Bashiru Ally, amewataka Watanzania kutumia uwezo wa kuhifadhi vitabu vitakatifu kuongeza ubunifu katika nyanja ya sayansi na teknolojia na nyingine ili kuendeleza jamii kwa kuipatia maendeleo stahiki.Dk Bashiru alitoa mwito huo katika kata ya Pahi wilayani Kondoa mkoani Dodoma, wakati wa mashindano ya kuhifadhi Kurani yaliyowashirikisha wadau kutoka maeneo mbalimbali nchini.Alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa katika kuwekeza kwenye elimu kwa watoto, kwa kuwa watoto wakisoma si tu wanajengewa maarifa lakini pia wanaunganishwa na hivyo kuwa chachu ya kuweza kuisaidia jamii inayowazunguka.Mratibu na Mwandaaji wa mashindano hayo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa, Dk Ashatu Kijaji, alisema kuwa lengo la mashindano hayo ya kuibua vipaji vya watoto vya kusoma Kitabu Kitukufu cha Kurani ni kuwajengea uwezo wa kuwa na ujasiri katika kueleza wanayoyaamini yakiwemo mambo mazuri ambayo yanafanywa na serikali.Kwa upande wake, Naibu Spika Dk Tulia Ackson alisema kuwa kazi zinazofanywa na Dk Kijaji, ni za kupigiwa mfano hasa kwa wanawake na akawataka wazazi katika Wilaya ya Kondoa kumuunga mkono kwa kushiriki kikamilifu katika mikakati ya kuinua elimu katika eneo hilo.Aidha, aliwataka kuhakikisha wanawapeleka watoto katika makambi yaliyo na lengo la kuongeza ufaulu wa wanafunzi.Mgeni asmi katika mashindano hayo, Shehe wa Mkoa wa Dodoma, Mustapher Shabaan, aliwapongeza vijana walioshiriki mashindano hayo na kuonesha umahiri mkubwa wa kuhifadhi Kurani na kuwataka waumini wa Kiislamu kusoma na kukielewa kitabu hicho kitukufu.Alifafanua kuwa kitabu hicho kimejaa elimu na maarifa mengi yatakayowasaidia kuenenda vyema katika jamii na kupata thawabu kutoka kwa Mungu. | 3 |
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amezindua mfumo wa usambazaji wa dawa, maarufu kama 'Jazia.Ameagiza dawa zipatikane si chini ya asilimia 98 katika kila kituo cha afya wakati wasambazaji walioshinda zabuni watakapokua wameanza kazi.Tukio la uzinduzi limekwenda sanjari na kusaini mikataba ya usambazaji kati ya Halmashauri zote za mkoa wa Dar es Salaam na washitiri (wasambazaji) ambao ni Bahari Pharmacy na Umoja Pharmaceuticals watakaosambaza dawa jijini humo.Mfumo huo ni maalumu kusambaza dawa kuanzia pale inapoishia (inaposhindwa kufika) Bohari ya Dawa nchini (MSD) na washitiri watatakiwa kuzingatia bei za Bohari Kuu au chini yake kwa kipindi chote cha mkataba.Imefahamika kuwa, mfumo huo hautaathiri bajeti ya serikali kuu kwa sekta ya afya, na kwamba, washitiri watakua wakilipwa kutokana na vyanzo vya vituo vya afya."Nimefurahishwa na jitihada zilizofanywa na kufanikisha kuwepo wa mfumo huu maana nimesikia huko nyuma hadi makampuni ya umeme yalikua yakipewa tenda ya kusambaza dawa. Hii ni kuonesha kwamba watu wamefanya vifo na matatizo ya watu kuwa uwekezaji wao. Ni hatari...," amesema Waziri Jafo.Ameagiza zabuni zitangazwe na washitiri wapatikane katika mikoa yote kabla ya mwezi huu kuisha. | 3 |
Na JANETH MUSHI – ARUSHA WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amewataka wapigakura wa Jimbo la Arusha Mjini kutovunjika moyo na kuwaeleza kuwa Mbunge wao Godbless Lema (Chadema) ambaye yuko mahabusu ya Gereza Kuu la Kisongo mjini hapa, atavuka salama katika kipindi kigumu anachopitia. Alidai kuwa watu wenye roho mbaya wako wengi kwani hata yeye walimwombea kifo muda mrefu, lakini hadi sasa anadunda. Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), aliyasema hayo jana katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa Kata ya Mateves, Wilaya ya Arumeru mkoani hapa baada ya wananchi kupaza sauti wakimuuliza juu ya hali ya Lema. Lema anashikiliwa katika gereza hilo kwa zaidi ya miezi miwili tangu alipokamatwa Novemba 2, mwaka jana katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma na kushtakiwa kwa uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli. Lowassa alisema kuwa alienda gerezani na Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, kumwona Lema ambaye alidai kuwa afya yake ni njema ila anasumbuliaa na jambo linalofanywa na Serikali ambalo hata wao hawalielewi. “Tatizo nikisema maneno wanaandika sana kwenye magazeti, halafu wakubwa wanachukia, tulienda na Sumaye kumwona Lema, ana afya nzuri ila anasumbuliwa na jambo linalofanywa na Serikali ambalo hatulielewi, siwezi kuzungumzia sana kwa kuwa suala hili liko mahakamani. “Tunalielewa tatizo lake, tuko pamoja na Lema na wapigakura wake, tunamwombea Mungu amsaidie avuke salama, hawa watu wenye roho mbaya wako wengi, walisema nitakufa, lakini nadunda,” alisema Lowassa. Akizungumzia uchaguzi huo mdogo unaotarajiwa kufanyika Januari 22, aliwataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Vijijini kusimamia kikamilifu uchaguzi huo ili mgombea wao Abel Jeremiah aweze kushinda. Lowassa aliwahakikishia wananchi wa kata hiyo kushinda, kwani wamemsimamisha mgombea ambaye ataweza kusimama na kutatua kero zao zinazowakabili. “Madiwani simamieni uchaguzi huu vizuri, ila mkilala mkanywa mbege tumekwenda na ninawakabidhi hapa kwa kiapo na ninawahakikishia tutashinda zaidi, ndiyo maana nimekuja kwenye uzinduzi wa kampeni hizi, nawaomba mumpe mgombea wa Chadema kura zote. “Tunajenga hoja kwani kura zinapatikana kwa hoja, tukatae kuibiwa kura ndugu zangu kwani chama chetu kina nguvu sana, Mateves msilale bado mapambano, lindeni kura ili tushinde kwa kishindo,” alisema. Lowassa alisema atahakikisha kuwa mgombea wao akishinda atatatua kero mbalimbali ikiwamo maji. “Nawaahidi maji yasipokuja simameni barabarani mnizuie, nitakwenda nyumbani kwake kumtoa kwa mke wake ili atatue kero hiyo kubwa,” alisema Lowassa. Awali akiomba kura kwa wananchi, Jeremiah aliahidi kusimamia mikopo kwa makundi ya akina mama na vijana kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Vijijini pamoja na kutatua kero ya maji. Awali Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ambaye pia ni Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, aliwaagiza madiwani wa Chadema, Jimbo la Arumeru Magharibi kuhakikisha mgombea huyo anashinda vinginevyo wajiuzulu. Naye Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, alisema kuwa mahakama ilimvua udiwani mgombea wa CCM baada ya kuthibitisha kuwa alitoa taarifa za uongo kuhusu Abel, hivyo kuwaomba wananchi kutomchagua tena. “Mahakama ilibaini kuwa madai ya Abel kudaiwa kuua siyo ya kweli, leo CCM wanaleta mgombea ambaye mahakama ilimuona ni muongo, uongo ni mbaya, akiwa kiongozi atasema yapi ya ukweli,” alisema na kuwataka wananchi kumchagua mgombea wa Chadema. | 3 |
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ipanga kutekeleza miradi saba mikubwa jijini humo, ambapo katika mwaka huu wa fedha 2019/20 litaanza na utekelezaji wa miradi miwili.Miradi itakayotekelezwa katika mwaka huu wa fedha ni kujenga kitega uchumi katika mji wa serikali Ihumwa na ujenzi wa hoteli ya kisasa ya nyota nne katikati ya jiji hilo. Mkurugezi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi, alisema hayo wakati wa utiaji saini na wakandarasi watakao tekeleza miradi hiyo miwili, Mohamed Builders na Setcol ya China, katika mradi wa kitega uchumi na hoteli ya nyota nne kwa mfuatano.Alisema kutokana na halmashauri hiyo kuongoza katika ukusanyaji mapato ghafi nchini katika mwaka wa fedha 2017/18 na 2018/19 ambayo yalitokana na upimaji wa viwanja ambacho si chanzo cha kudumu, imeamua kujiongeza na kupanua wigo wa mapato.Alisema halmashauri hiyo imebuni miradi mikubwa ya uwekezaji ili kuwa na vyanzo vya kudumu vya mapato ya ndani badala ya kutegemea viwanja ambavyo si vynzo vya kudumu.Kunambi alisema ili kufanikisha miradi hiyo, halmashauri hiyo katika mwaka wa fedha 2018/19 iliandaa michoro ya miradi ya uwekezaji saba, ambayo kati yake miwili inaanza kutekelezwa mwaka huu na mitano itatekelezwa miaka ijayo.Alitaja miradi iliyoandaliwa michoro itakayotekelezwa baadaye ni wa maduka makubwa utakaojulikana kama Nyerere Square Plaza ambao utajengwa katika eneo la Sunja na Victoria jijini hapa na ujenzi wa maduka makubwa (Malls) eneo la NCC.“Pia ujenzi wa nyumba ya kupanga katika eneo la NCC na ujenzi wa kitega uchumi mkabala na Msikiti wa Nunge uliopo katikati ya jiji pamoja na ujenzi wa maduka, ofisi na kumbi za mikutano karibu na NKClub ya zamani,” alisema.Alisema miradi hiyo imepangwa kutekelezwa kwa kutumia mapato ya ndani, mikopo kutoka katika benki na ruzuku ya fedha za miradi ya kimkakati kutoka serikali kuu.“Lengo la miradi hiyo ni uwekezaji pamoja na kuongeza mapato ya halmashauri na kupunguza utegemezi kutoka serikali kuu na kuongeza ajira kwa wananchi wa Dodoma,” alisema.Alisema lengo jingine ni kuongeza na kutoa huduma bora kwa wananchi, kupendezesha na kuboresha jiji la Dodoma na kupunguza umasikini na kuongeza kipato cha mwananchi mmoja mmoja.Naye Meya wa Jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe, alisema pamoja na jitihada za halmashauri kuwekeza katika miradi hiyo, wanaiomba serikali kuchangia katika uwekezaji huo ili kulisaidia jiji hilo kujenga mandhari nzuri ya makao makuu ya serikali. | 3 |
MKUTANO wa 18 wa Bunge la Kumi na Moja pamoja na kupokea na kujadili taarifa za mwaka za Kamati za Kudumu za Bunge pia utakabidhi majoho kwa maspika wastaafu watatu waliyokuwa wakiyatumia wakati wakiongoza Bunge.Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma, Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema maspika watakaokabidhiwa majoho hayo ni pamoja na Pius Msekwa, Samuel Sitta kwa niaba yake mke wake Margareth Sitta na Anne Makinda."Katika Mkutano huu 18 wa Bunge kutakuwa na shughuli ya kukabidhi majoho kwa maspika wastaafu Pius Msekwa, Samuel Sitta (Marehemu) ambapo joho alilotumia litapokelewa na mke wake, Margaret Sitta kwa niaba ya familia, na Anne Semamba Makinda," alisema.Spika Ndugai alisema shughuli hiyo itafanyika leo Januari 28, 2020 katika kikao cha kwanza cha Mkutano wa 18 wa Bunge mara baada ya kipindi cha maswali," alisema.Alisema katika mkutano huo ambao ni mahususi kwa ajili ya Bunge kupokea na kujadili taarifa za mwaka za kamati, pia katika mkutano huo maswali 125 ya kawaida yanatarajiwa kuulizwa na wabunge.Pia wastani wa maswali 16 ya papo kwa papo yataulizwa kwa Waziri Mkuu Alhamisi Januari 30 na Februari 6, mwakak huu.Ndugai alisema katika mkutano huo pia Bunge litajalidi na kupitisha miswada miwili ya sheria ukiwemo wa marekebisho ya sheria mbalimbali namba Nane wa 2019 na muswada wa sheria ya Usuluhishi wa mwaka 2020.Katika muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho sheria 14 zikiwemo ya haki za watoto, mamlaka ya sheria za serikali za mitaa za wilaya na mikoa, ya uvuvi na ya viwanda vya nyama.Pia katika mkutano huo taarifa za kazi za mwaka mzima za kamati 15 zitawasilishwa kwa mujibu wa masharti ya Kauni ya 117 (5) ambazo ni Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali, Hesabu za serikali za mitaa, Uwekezaji na Mitaji ya Umma, Kamati ya Bajeti na Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira."Kamati ya Miundombonu, Nishati na Madini, Ardhi Maliasili na Utaliii, Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, Huduma na Maendeleo ya Jamiii, Kamati ya Masuala ya Ukimwi, Sheria Ndogo na Katiba na sheria, kamati ya tawala na serikali za mitaa na mambo ya nje, ulinzi na usalama.Mkutano huo wa 18 wa Bunge la kumi na moja unaanza leo Januari 28 hadi Februari 7, mwaka huu jijini Dodoma. | 3 |
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Bodi ya muda ya Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi (WETCU), Hassan Wakasuvi alipozungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kurejea kutoka nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu ya mguu.Wakasuvi alisema kwa muda mfupi ambao Bodi hiyo imekuwepo madarakani imefanikiwa kufanya mambo mengi likiwemo kusimamia na kuhakikisha wakulima wananufaika na zao hilo kwa kuuza kwa bei yenye tija.Alisema kuwa katika msimu wa kilimo wa mwaka 2012/2013 mbolea aina ya NPK iliuzwa kwa dola 53.90 ambapo msimu wa mwaka 2013/2014 iliuzwa kwa dola 51.35 ikiwa na tofauti ya dola 2.55.Aidha alisema kuwa mbolea aina ya CAN katika msimu wa 2012/2013 iliuzwa kwa dola 38.60 ambapo msimu wa2013/2014 iliuzwa kwa 33.30 ikiwa na tofauti ya dola 5.30.Aliendelea kufafanua kuwa mbolea aina ya UREA katika msimu wa kilimo wa 2012/2013 iliuzwa kwa dola 46.60 na msimu wa mwaka 2013/2014 kuuzwa kwa dola 34.85 sawa na tofauti ya dola 11.75.Pia alisema Confidor ya pakiti katika msimu wa mwaka 2013/2014 iliuzwa kwa dola 4.46 ambapo katika msimu wa 2013/2014 iliuzwa kwa dola 2.88 ikiwa na tofauti ya dola 1.58.Alisema dawa aina ya Yavikonyo katika msimu wa 2012/2013 iliuzwa kwa dola 28.94 na 2013/2014 ikiuzwa kwa dola 20.60 sawa na tofauti ya dola 8.34.Wakasuvi alisema katika kipindi hicho cha bodi ya muda pia walifanikiwa kuokoa fedha kiasi cha dola za Marekani 236,088.72 sawa na Sh 4,632,844,632 kutokana na tofauti ya bei ya msimu wa kilimo katika mwaka 2012/2013 na 2013/2014. | 5 |
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Zainab Chaula amesema wakuu wote wa vyuo vya afya, ambao hawajathibitishwa au hawakupewa barua za kukaimu, watapewa barua za kuthibitishwa ifi kapo Jumatatu.Dk Chaula alisema hayo wakati wa kufungua mkutano wa siku tatu wa wakuu wa vyuo vya afya vya serikali, waliokutana jijini hapa na kuongeza kuwa hakuna sababu ya wakuu hao kukata tamaa. “Kwa yule ambaye anatakiwa kuthibitishwa, atathibitishwa na yule ambaye hana barua ni lazima wote kila mmoja atapewa barua ifikapo Jumatatu, hakuna anayetakiwa kukaimu milele.Kikubwa ni kujiamini na huna sababu yoyote ya kukata tamaa.” Aliongeza kuwa: “Na kwa watumishi wenye sifa ya kupandishwa madaraja nao watapandishwa,” alisema Dk Chaula baada ya kupokea taarifa ya wakuu wa vyuo.Awali akiwasilisha taarifa ya wakuu wa vyuo, Mkuu cha Chuo cha Maofisa Tabibu Songea, Dk Geofrey Mdede alisema kumekuwepo na changamoto kwa waliopewa cheo cha madaraka ya mkuu wa chuo, kukaimu kwa muda mrefu bila kuthibitishwa huku wengine wakiwa hawana hata barua za kukaimu. “Wapo wengine wanakaimu nafasi hiyo kwa muda mrefu na kuna wengine wanakaimu kwa zaidi ya miaka 10 mpaka wamestaafu, pia pamoja na kukaimu wapo ambao wamefanya kazi hiyo muda mrefu hata barua za kukaimu hawana,” alisema.Alisema changamoto nyingine ni kwa watumishi kutopandishwa madaraja kwa wakati, kwani baadhi wana zaidi ya miaka 10. “Hata kwa wale ambao wamefikia hatua ya kupanda madaraja, kuna vigezo vilivyoonekana kuongezeka, kwa mfano kuwa na machapisho angalau matatu,”alisema. Mdede alisema pia vyuo vinakabiliwa na changamoto ya rasilimali watu hasa uhaba mkubwa wa walimu, wanaotakiwa kufundisha masomo mbalimbali, wahasibu, maofisa wa Tehama na watumishi wa kada zingine kama makatibu afya, ofisa ugavi, madereva, wahudumu, wakutubi na watunza kumbukumbu.“Upungufu huu umeleta madhara katika udahili, kama tunavyoshuhudia baadhi ya vyuo kuzuiliwa kufanya udahili mwaka jana na mfano mzuri ni Chuo cha Tabibu wa Meno Mbeya ambacho kina walimu wawili tu,” alisema. Alisema changamoto nyingine ni maslahi duni ya watumishi, kukosekana kwa motisha, madai ya malimbikizo, ukosefu wa watumishi na ukosefu wa mafunzo kwa watumishi.Aidha, Dk Chaula pamoja na kupokea changamoto kutoka kwa wakuu hao aliwataka kutumia mkutano huko kujadili changamoto zinazowakabili na kuja na mikakati ya kuzitatua. Pia aliwataka wakuu wa vyuo hivyo kuwa wabunifu katika kuendesha vyuo na kuongeza makusanyo ya ndani, ambayo watayatumia kuondoa baadhi ya changamoto katika taasisi zao. Pia Dk Chaula alimuagiza Mkurugenzi wa Mafunzo wa Wizara ya Afya kukifufua upya Chuo cha Mbozi kilichoanzishwa mwaka 197, ambacho kwa takribani miaka miwili hakijafanya udahili wa wanafunzi kwa sababu ya ukosefu wa walimu. | 3 |
MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba jana walilipa kisasi baada ya kuifunga Mashujaa ya Kigoma kwa bao 1-0 katika mchezo wa kirafi ki uliofanyika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.Ushindi huo wa Simba ni sawa na kulipa kisasi baada ya vigogo hao wa soka nchini kufungwa 3-2 na kutolewa katika michuano ya Kombe la Shirikisho na timu hiyo ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam msimu uliopita.Katika mchezo huo ulioshuhudiwa na watazamaji wengi kwenye uwanja huo, bao hilo pekee la Simba lilifungwa katika dakika ya 56 na mchezaji wa kimataifa wa Sudan, Sharaf Shaiboub aliyeunganisha mpira wa pasi ndefu ulipigwa na kiungo wa kati Said Ndemla.Aidha, huo ni ushindi wa pili mfululizo kwa Simba baada ya juzi kuibuka na ushindi kama huo kwenye mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Bandari FC ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Katika mchezo mwingine wa kirafiki jana, Azam FC ilifunga African Lyon kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi, huku mabao yake yakifungwa na Iddi Kipagwile na Joseph Mahundi.Yanga nayo iliifunga Friends Rangers kwa mbaoa 4-3 katika mchezo wa mazoezi kwenye Uwanja wa Polisi Kurasini wakijiandaa kwa mechi ya mtoano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Pyramids ya Misri Oktoba 27 CCM Kirumba Mwanza. | 4 |
KILIMANJARO Queens imekuwa timu ya kwanza kutinga nusu fainali ya michuano ya Wanawake ya CECAFA inayoendelea kwenye uwanja wa Chamazi Complex Dar es Salaam.Hiyo inatokana na vipigo inavyoendelea kuvitoa katika kundi A, ambapo hadi sasa wameweza kushinda mechi zote mbili na kufunga mabao 13. Kilimanjaro Queens ambao ndiyo mabingwa mara mbili wa michuano hiyo, huu ni msimu wa tatu na kocha wake, Bakari Shime amepania kuhakikisha wanatwaa kwa mara ya tatu taji hilo ili kuweka rekodi ya kipekee kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.Katika mchezo wa jana Kilimanjaro Queens iliingia kwa kuwashangaza wapinzani wao baada ya kocha Shime kubadilisha asilimia kubwa ya kikosi chake kilichocheza mechi ya kwanza dhidi ya Sudani Kusini na kuibuka na ushindi wa mabao 9-0, mmoja wao akiwemo nahodha Asha Rashid na Fatma Abdallah.Mabao ya Kilimanjaro Queens katika mchezo wa jana dhidi ya Burundi yalifungwa na Donisia Daniel aliyefunga mabao mawili dakika ya 34 na 65, Asha Mwalala dakika ya 72 na Mwanahamisi Omary dakika ya 86.Mbali na Kilimanjaro Queens timu nyingine inayofanya vizuri kwenye mashindano hayo ni timu ya taifa ya Uganda ambayo Jumapili iliibuka na ushindi wa mabao 13-0 dhidi ya Djibout na pengine inaweza kuwa timu inayoweza kutoa changamoto kwa timu yoyote kati ya zinazoshiriki mashindano hayo.Uganda ambayo ipo kundi B, pamoja na mataifa ya Kenya, Ethiopia na Djibout ni miongoni mwa nchi ambazo imewahi kutolewa na Tanzania katika hatua ya nusu fainali mwaka 2016 jijini Kampala.Wakati hali ikiwa hivyo kwa Kilimanjaro Queens, mambo sio mazuri kwa ndugu zao, Zanzibar Queens ambao walikubali kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Sudan Kusini ikiwa ni muendelezo wa matokeo mabaya kwa timu hiyo kwenye mashindano hayo kwani kwenye mchezo wao uliopita, walipokea kipigo kama hicho kutoka kwa timu ya taifa ya Burundi. | 4 |
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inajenga na kuboresha mtandao wa miundombinu ya barabara, reli ya kisasa na uwanja wa ndege ili kuzifikia huduma muhimu kwa urahisi.Katika mkakati huo wa kuunganisha maeneo muhimu ipo Ikulu ya Chamwino na Mji wa Serikali zinaunganishwa na huduma za stendi na soko la kimataifa.Akizungumza na wabunge wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa Jiji, Godwin Kunambi amesema anataka kujenga mawasiliano ya vyombo vya usafiri angani na ardhini.Alisema miundombonu itakayounganishwa ni pamoja na itaunganishwa maeneo muhimu ni barabara za lami zikiwemo za mzunguko na kuunganisha kupita kwenye stendi na soko la kimataifa pamoja na uwanja wa burani.Alisema mtu akisafiri kwa reli ya kisasa (STG) kutoka Morogoro ataingia Dodoma kupitia Ihumwa ambayo itaunganishwa na barabara ya lami kuu ya Morogoro-Dodoma umbali wa kilometa chache.“Msafiri wa ndege atashuka katika uwanja wa Msalato na kusafiri umbali wa kilometa 30 kwa basi hadi kufika stendi kuu na kuchukua usafiri wa kwenda mikoa mbalimbali nchini,” amesema.Kunambi alisema wafanyakazi wa Ikulu Chamwino wakiwata wanaweza kutasafiri kwa usafiri wa mabasi umbali wa kilometa saba kwenda mji wa serikali na kuamua kusafiri kwa barabara au reli katika kituo cha Ihumwa kwenda popote.Kunambi alisema Halmashauri ya Jiji imetenga zaidi ya Sh bilioni 77.7 kwa ajili ya uboreshaji miundombinu hiyo muhimu jijini ili kulifanya jiji hilo lilingane na hadhi ya majiji makubwa duniani.Alisema katika kuboresha miundom mbinu ya barabara, halmashauri imetenga Sh bilioni 18.34 kwa ajili ya kumlipa mkandarasi Chico kukamilisha barabara hizo hadi sasa imelipwa Sh bilioni 4.7.“Mkataba wa uboreshaji barabara za mchepuko ulisainiwa Julai 1, mwaka jana ni mradi wa miezi 15 unatazamiwa kukamilika 30 Septemba na kuanza kutumika,” alisema.Alisema katika kuhakikisha huduma za usafiri zinaenda pamoja na huduma za chakula, katika kituo cha Mabasi, stendi itakuwa na maduka maalumu ambayo yatafanya kazi saa 24 na kwa siku saba. Alisema msafiri atakuwa na nafasi ya kutumia mabasi madogo kutoka stendi na kwenda kupanda treni ambayo ifikapo 2021/22 itakuwa imekamilika kutoka Morogoro hadi Dodoma.“Kukamilika kwa reli katika kituo cha Ihumwa kutaunganishwa na stendi ya mabasi ya mjini ambayo yametengewa eneo la ekari 30,” alisema.Alisema mtu akishuka kwenye treni anaweza kupanda basi la jiji (kutumia umeme) kuchuka stendi kwenda Arusha au Singida au kupanda ndege katika uwanja wa Msalato na kutakuwa na basi kilometa 30 kufika uwanja huo.Kutokana na kuwepo kwa miradi hiyo, wananchi 580 wamepata ajira, wakiwemo wanaume asilimia 70 na wanawake asilimia 30 ya watu wanaofanya kazi katika stendi ya Dodoma.Kunambi alisema, wijana wa mji huo ambao hana uwezo wa kuuza saruji au nondo ataweza kuuza nguvu zake. Mradi hii ya Benki ya Dunia inagharimu Sh bilioni 77.7 na ajira zote zinakwenda kwa vijana wa Dodoma. | 3 |
Samwel Mwanga – Meatu Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Mzee Mkongea amewataka wakandarasi wanaotekeleza
miradi ya maji nchini kuikamilisha kwa wakati uliopangwa kwa lengo la
kuwanufaisha wananchi. Ametoa kauli hiyo leo Mei 23, mara baada ya kukagua mradi wa maji katika
kijiji cha Itinje ulioko wilayani humo ambapo amesema kuwa miradi mingi ya maji
huwa haikamiliki kwa wakati huku akitolea mfano wa mradi huo ambao ulianza kutekelezwa
tangu juni 2014 lakini hadi sasa haujakamilika. “Miradi mingi ya maji inayosimamiwa na serikali haikamiliki kwa
wakati na wakati mwingine fedha zinazotengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo
hutumika hovyo, mfano ni huu mradi ambao tuliopo sasa ulianza mwaka 2014 na
ulitakiwa ukamilike juni 2016 lakini hadi leo haujakamilika na moja ya sababu
ni mkandarasi kutokuwa na watalaamu wa kutosha, mtatoaje zabuni kwa mtu asiye
na wataalamu wa kutosha na haya ni matumizi mabaya ya fedha za serikali?”
amesema. Aidha amemtaka mkandarasi anayejenga mradi huo kupima vifaa vya ujenzi ambavyo
ni nondo na zege katika kipindi cha majuma matatu na kisha apatiwe taarifa
sehemu yoyote watakayokuwepo huku akiwataadharisha viongozi wa halmashauri
kutoa zabuni kwa upendeleo. Awali akisoma taarifa ya mradi huo, Mhandisi wa maji wilayani humo, Sylvester
Pauline alisema mradi huo umelenga kuhudumia wakazi wapatao 3,962 na utagharimu
kiasi cha Sh Milioni 450.26 hadi kukamilika. | 3 |
Yanga itacheza na APR ya Rwanda wiki ijayo na kikosi cha mabingwa hao wa Tanzania kinatarajiwa kuondoka nchini Jumatano ijayo kwenda Kigali, Rwanda kuwakabili maafande hao wa jeshi la Rwanda katika mchezo wa kwanza wa mchezo wa raundi ya kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika.Aliliambia gazeti hili jana kwa njia ya mtandao kuwa, ushindi katika mchezo wa kesho utakuwa na maana kubwa kwao Yanga hasa kwa kuwa mikakati yao ni kufanya vizuri katika michuano yote wanayoshiriki hivi sasa.“Ni mchezo mgumu kwa timu zote mbili, lakini hatuna budi kupambana kupata ushindi utakaotupatia nguvu kuelekea kutetea ubingwa wetu, lakini pia kuwafuata APR, tukiwa na matumaini ya ushindi kutokana na kikosi kuwa na ari ya kufanya vizuri,” alisema Pluijm.Alisema katika mazoezi ya wiki hii yanayoendelea kisiwani Pemba, amejitahidi kuwafundisha wachezaji wake mbinu tofauti na zile za siku zote akiamini zitawasaidia kupata matokeo mazuri katika mechi hizo mbili zinazowakabili.Alisema Azam ni moja ya timu ambayo imekuwa ikiwasumbua mara kwa mara, lakini safari hii amepania kuipa kipigo kitakachowavuruga kabisa.“Nafurahi kuona vijana wangu wote wakiwa katika hali nzuri kuelekea katika mchezo huo kitu ambacho kinanipa faraja ya kutimiza kwa asilimia kubwa kile ambacho tumekikusudia lengo letu ni pointi tatu ambazo zitatupa uhakika wa ubingwa,” alisema.Pambano hilo linasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini ili kuona ni timu gani itaon doka na ushindi na kujiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa msimu huu.Yanga na Azam ndizo zilizo kileleni mwa ligi, zote zikiwa na pointi 46 baada ya kushuka dimbani mara 19, lakini Yanga iko juu kutokana na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa. | 4 |
Akizungumza baada ya kutia saini makubaliano hayo jana, Mkurugenzi wa Azam TV, Tido Muhando alisema wameingia makubaliano na Clouds Media ili kuwaonesha watu wasioweza kufika katika viwanja kushuhudia mashindano hayo.“Tunawaahidi Clouds Media na Watanzania tutafanya kazi nzuri kwani sisi ndio kituo bora kwa urushaji wa matangazo hasa soka hilo halina ubishi,” alisema Tido. Naye Mratibu wa Ndondo Cup, Shafii Dauda aliwashukuru Azam Media kuwa sehemu yao katika kuendesha mashindano hayo kwa miaka minne mfufulizo.“Lengo la mashindano ni kutengeneza daraja kwa vijana wenye vipaji ili waonekana na wasajiliwe na timu za madaraja ya juu hivyo tunaishukuru Azam Media kuwa sehemu yetu kufanikisha ndoto za vijana,” alisema Shafii.Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam, Almas Kasongo aliishukuru Azam Media na Clouds Media kwa kusaidia kuendeleza michezo Dar es Salaam. “Tunafurahi kuona soka likichezwa katika mkoa wetu kwani mnasaidia kutekeleza moja ya majukumu yetu hivyo nawaahidi mashindano haya yatasimamiwa kwa weledi mkubwa,” alisema Kasongo.Droo ya makundi ya mashindano hayo inatarajiwa kuchezeshwa leo katika viwanja vya Escape One, Kinondoni ambapo timu 32 zitakuwa kwenye bakuli moja. Timu hizo ni Vituka FC, Twiga International, Kigoma Kombaini, Stimtosha, Tandavamba, Black Six, Ukwamani, Ndanda Investment, Miami, Mpakani Kombaini na Kibo Kombaini.Vijana rangers, Goroka FC, Burudani, Polisi DSM College, Faru jeuri, Boom FC, Temeke Market, Temeke Squad, Tabata United, Misosi, Keko Furniture na Buguruni United. Nyingine ni Goms United, Kigogo Kombaini, Wauza matairi, Shelaton, Makuburi, Kibada One, Kauzu FC, Mlalakuwa Rangers na Madiba FC. | 4 |
NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (pichani) amezitaka kampuni zinazotakiwa kulipa fi dia katika maeneo ya uchimbaji kufanya hivyo kwa wakati ili kuondoa migongano na wananchi.Nyongo alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM) aliyetaka kujua lini serikali itawalipa fidia wananchi ambao wamefanyiwa tathimini lakini hawajalipwa fidia yao kwa miaka mingi? Nyongoi alisema Sheria ya Ardhi Namba 4, 1999 inataka waliothaminiwa ardhi kupisha maeneo kulipwa fidia ndani ya miezi sita.Alisema, baada ya hapo mwekezaji anatakiwa kulipa kwa riba na ikizidi miaka inatakiwa kufanyika uthamini upya kwenda na wakati. “Hivyo nizitake kampuni ambazo zinatakiwa kulipa fidia kupisha maeneo ya uchimbaji kufuata sheria kwa kuwalipa wananchi kwa wakati unaoelekezwa na sheria,” alisema.Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Upendo Peneza (Chadema) alisema wizara kupitia Ofisi ya Madini Mkoa wa Geita itasimamia na kukagua eneo la mtaa wa Mgusu.Katika swali la msingi, Peneza alisema: “Wananchi wa Mtaa wa Mgusu wanaoishi ndani ya mipaka ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita Gold wanaathirika na uchafuzi wa mazingira wa taka zinazomwagwa karibu na wananchi.” Peneza alitaka kujua ni lini serikali itatoa agizo kwa Mgodi wa Geita kulipa wananchi fidia ili watoke katika eneo lililomilikishwa mgodi. Nyongo alisema wananchi wa mtaa wa Mgusu wanajishughulika na uchimbaji mdogo madini.“Hata hivyo, tathimini ya mazingira iliyofanywa na mgodi wa GGM haioneshi uwepo madhara yanayohitaji kuhamishwa kwa wananchi wa kitongoji hicho,” alisema Waziri Nyongo. Alisema Sheria ya Madini ya Mwaka 2010, Kifungu cha 96(1) na 97(1) (a) na (b) vinaeleza fidia inapaswa kulipwa kwa mujibu wa Sheria. Alisema mwekezaji anatakiwa kuanza kuchimba madini baada ya kushauriana na mamlaka za serikali za mtaa husika na kujiridhidhsha juu ya madhara yanayoweza kusabishwa na uchimbaji huo.Aidha, Nyongo alisema Mtaa wa Mgusu uko Kilometa 4,5 kutoka eneo la uchimbaji la Nyamulilima Star na Commet la GGM ambapo uchimbaji unaendeshwa njia ya chini kwa chini. “Kwa umbali huo ni vigumu kwa taka ngumu kufika katika mtaa huo, hata hivyo, ukingo wa miamba isiyo na madini umewekwa kuzuia miamba hiyo kutoka nje ya eneo la uchimbaji.” | 3 |
KIFO cha bilionea maarufu nchini Tanzania na Afrika Mashariki na mmiliki wa Makampuni ya IPP, Dk Reginald Mengi, kimewashtua wengi, huku akiwa ameacha pengo kubwa katika maeneo ya biashara na vyombo vya habari.Dk Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni hayo ya IPP, alifariki dunia usiku wa kuamkia jana Dubai katika Falme za Kiarabu baada ya kuugua muda mfupi. Mfanyabiashara huyo anayemiliki vyombo mbalimbali vya habari amefariki, ikiwa ni takribani miezi sita tangu kifo cha aliyekuwa mtalaka wake, Mercy Mengi aliyekutwa na umauti akiwa Afrika Kusini.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia yake, Dk Mengi aliyezaliwa mwaka 1942 mkoani Kilimanjaro, alikutwa na umauti wakati akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mfupi.Dk Mengi, mwandishi wa kitabu cha I Must, I Can, I Will kinachoelezea safari ya maisha ya dhiki akiwa mtoto hadi kuwa msomi mkubwa wa fani ya uhasibu na kisha tajiri, maisha yake yatakumbukwa na mambo mbalimbali, yaliyosaidia kukuza uchumi wa Taifa sambamba na misaada ya kijamii kwa watu wasio na uwezo.Rais Magufuli amlilia Rais John Magufuli ametuma salamu zake za rambirambi kwa familia ya Dk Mengi na Watanzania wote kutokana na kifo hicho, huku akielezea mambo mengi yaliyofanywa na Mengi wakati wa uhai wake. Kupitia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Rais Magufuli alisema ataendelea kumkumbuka Mengi kwa mchango wake katika maendeleo ya taifa lake.Kupitia ukurasa huo, Rais Magufuli ameandika “Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Mzee na Rafiki yangu Dk Reginald Mengi. Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya Taifa letu na maono yake yaliyopo katika kitabu chake cha I Can, I Will, I Must. Poleni wanafamilia, wafanyakazi wa IPP na Jumuiya ya Wafanyabiashara”.Viongozi wazungumza Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas pia ameandika kupitia ukurasa wake wa Twitter akitoa salamu hizo za rambirambi, akinukuu kauli yake aliyowahi kuitoa wakati wa uhai wake. “Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mwenyekiti wa IPP, Mzee Reginald Mengi. Kama alivyopata kusema yeye mwenyewe siku za uhai wake kuwa watu wanaoacha alama hawafi, basi mawazo, falsafa, ubunifu na kujitoa kwake vitaendelea kuishi nasi,” alisema Dk Abbas kupitia ukurasa wake huo wa mtandao wa kijamii.Mbali na hao, kifo cha Mzee Mengi kimewagusa watu mbalimbali akiwemo bilionea na mfanyabiashara mwenzake, Mohammed Dewji maarufu Mo na Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ambaye aliandika kupitia ukurasa wake kuwa amejifunza mengi kupitia kwa mfanyabiashara huyo, ambaye kwake alikuwa rafiki, kiongozi na mzazi akimfundisha suala zima la kuwa kukata tamaa ni dhambi.Naibu Spika, Dk Tulia Ackson alitoa pole kwa familia na wafanyakazi wote wa IPP kutokana na msiba huo. “Ni wazi tumepata pigo kubwa ila Mwenyezi Mungu awasimamie na kuwapa nguvu katika kipindi hiki kigumu. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Amen,” alisema. Nao wabunge wameeleza kwa nyakati tofauti, hisia zao kuhusu msiba huo, huku wengi wao wakielezea ushiriki wa Mengi wakati wa uhai wake katika kuendeleza vyombo vya habari na biashara nchini na ndani ya jumuiya ya Afrika Mashariki.Mbunge wa Viti Maalumu, Lucy Owenya (Chadema) alisema jumuiya ya wafanyabiashara, imempoteza mtu muhimu na alikuwa nguzo ya taifa. “Nimepokea kwa masikitiko sana kifo cha Dk Reginald Mengi, mimi namuita kaka yangu, kwanza kwenye jumuiya ya wafanyabiashara tumempoteza mtu muhimu sana aliyekuwa anapigania mambo ya kibiashara, sio hilo tu alikuwa mtu wa watu, kama taifa tumepoteza nguzo muhimu sana,” alisema.Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ (Chadema), alisema: “ nimeshituka sana na taarifa za msiba kwa sababu siku si nyingi nilikutana naye. “Dk Mengi ni mtu pekee aliyewavutia vijana wakati wa uhai wake akiwasihi kupambana na kuwataka wasikate tamaa katika ungozi na utafutaji. Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM) alisema Mengi ni alama ya matajiri wachache wenye unyenyekevu na hofu ya Mungu. “Ni matajiri wachache wenye utu, ameacha alama kubwa ya kusaidia watu masikini, watu wenye ulemavu na watu wenye mahitaji mbalimbali,” alisema.Alisema katika maisha yake, amekuwa kioo na mfano mkubwa sana wa kujinyenyekeza mbele za wenzake. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Muungano na Mazingira) ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, January Makamba (CCM), alisema: “ Nimepokea taarifa hiyo kwa masikitiko na mshtuko mkubwa na kwamba mzee Mengi ukizungumza historia ya biashara, vyombo vya habari hapa nchini jina lake lazima liwepo na amekuwa mwanzilishi au mtengeneza njia kwenye tasnia ya habari nchini.“Amegusa maisha ya watu wengi sana na kwa kweli tutamkosa kama taifa kwa sababu ametoa mchango mkubwa sana karibu katika kila eneo la uhai wa nchi yetu, kwenye uchumi kwenye biashara. Ni pigo kubwa kwa nchi”. Mbunge wa Vunjo, James Mbatia (NCCR-Mageuzi) alisema: “Niombe watanzania tuwe na utulivu wa ndani hasa wanatasnia ya habari nchini, sekta binafsi nchini na familia yake. “Nilibahatika kuwa na Mengi karibu sana na nilikutana naye Machi 17 mwaka huu alipoandaa chakula kwa ajili ya watu wenye ulemavu.Alinishirikisha mambo yake, inanibidi nitafakari zaidi. Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde (CCM) ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, alisema Mengi ameacha alama kubwa katika taifa la Tanzania. “Amekuwa ni mtu mwenye msaada kwa watu wengi wenye uhitaji na hasa watu wenye ulemavu watamkumbuka sana kwa mchango wake mkubwa wa kubadilisha fikra, mitizamo lakini pia kuwawezesha kiuchumi kufikia ndoto zao kwamba na wenyewe wanaweza wakasimama na kujitegemea,” alisema.Mbunge wa Bukene, Seleman Zedi (CCM) alisema Mengi alikuwa ni mtu aliyejali makundi kwenye jamii ambayo hayapewi nafasi, kama vile watu wenye walemavu, watu wanaoishi kwa mazingira magumu, albino na watu wa kawaida Mbunge wa Viti Maalumu, Upendo Peneza (Chadema) alisema kuwa Mengi amekuwa nguzo katika mafanikio yake kisiasa.“ Mimi nimemfahamu Mzee Mengi miaka mitano iliyopita wakati nagombea nafasi ya mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Taifa (Chadema) na aliniona nikihojiwa kwenye luninga na akaandika kwenye twitter kwamba ‘Ninamuangalia binti Upendo Peneza ni binti ambaye ana uwezo na uelewa mpana na kwangu mimi Upendo ni shujaa’.” “Baada ya ku-twitt alitafuta namba yangu mwenyewe akanipigia simu tukaongea, akanitia moyo na akaniambia niendelee na jitihada hizo za kutafuta nafasi katika uongozi mpaka hatimaye nikawa Mbunge,” alisema.Alisema twitter ya Mengi kwa kiasi fulani, ilimsaidia wakati wa kampeni kwa sababu nilikuwa naitumia wakati wa kuomba kura. Umoja wa Mataifa (UN) Kupitia ukurasa wa Twitter wa UN Tanzania, Umoja wa Mataifa (UN) umeandika, “Tumesikitishwa na taarifa za msiba wa Reginald Mengi. Tunaungana na Watanzania wote kuiombea familia ya marehemu katika kipindi hiki.Ubalozi wa Marekani Ubalozi wa Marekani pia kupitia taarifa yake, umeeleza kusikitishwa na kifo cha Dk Mengi, ukisema kuwa kwa siku za nyuma uliwahi kufanya kazi na marehemu na kushirikiana katika mambo mbalimbali. Taarifa iliyotolewa na ubalozi huo, ilisema kuwa utamkumbuka Dk Mengi kutokana na mchango wake katika ukuaji wa muda mrefu wa uchumi na maendeleo ya Tanzania.Ubalozi huo ulitoa pole kwa familia na kuungana na watanzania wote katika kuombeleza msiba huo mkubwa. Mpaka anaaga dunia, Mengi anatajwa kuwa mmoja wa matajiri wakubwa nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, akiwa na himaya ya biashara ya vyombo vya habari, kiwanda cha vinywaji baridi, kampuni za madini na kampuni zingine mbalimbali.Mwaka 2014 Jarida maarufu duniani la Fobes, lilimuorodhesha Mengi akiwa nafasi ya 45 kati ya matajiri 50 zaidi barani Afrika akiwa na utajiri wa Dola za Marekani 560 milioni sawa na zaidi ya Sh 1.2 trilioni za Tanzania. Wanahabari Waandishi wa habari wakiongozwa na Katibu wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Nevil Meena wamesema msiba wa Mengi ni pigo katika tasnia ya habari, kwani hakuna mwanahabari asiyetambua mchango alioutoa katika tasnia hiyo.Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uhuru Media, Ernest Sungura alisema kamati ya maandalizi, itatoa taarifa ya pamoja ya wanahabari kuhusu msiba huo. Alisema taarifa hiyo inayoandaliwa na nguli wa habari nchini, Theophil Makunga itaeleza kinaga ubaga mchango wa Dk Mengi katika kuikuza tasnia hiyo, ambaye kwa nafasi mbalimbali alizokuwa nazo, mbali ya umiliki wa vyombo kadhaa vya habari, kwa kiasi kikubwa alisimamia maendeleo ya tasnia hiyo.Uongozi wa makampuni ya IPP yanayomilikiwa na Dk Mengi, umetoa wasifu na historia ya Mengi. Hata hivyo, uongozi huo haujaeleza ni lini mwili wake utaletwa nchini na taratibu nyingine za mazishi. Baraza la EABC Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Baraza la Biashara Afrika Mashariki (EABC), imetoa pole kwa familia, marafiki na kampuni nzima ya IPP kwa msiba huo wa Dk Mengi.“Maneno hayawezi kuelezea pengo hili aliloliacha Dk Mengi ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa bodi ya EABC katika kipindi cha mwaka 2008/9. Alikuwa mchapakazi, mwenye upendo, kiongozi na kiongozi wa biashara,” ilisema taarifa iliyotolewa na bodi hiyo. Ilisema Dk Mengi alipokuwa mwenyekiti wa baraza hilo, alisisitiza juu ya ushirikiano wa kikanda kwa kuongoza mtazamo wa sekta binafsi ili kuingizwa katika Itifaki ya Soko la Pamoja la EAC.Historia yake fupi Dk Mengi alizaliwa Mei 29, mwaka 1942 katika familia duni mkoani Kilimajaro. Baadae alianzisha makampuni ya IPP ambayo yamekuwa yakihudumu nchini Tanzania na baadhi ya maeneo ya Afrika Mashariki. Kwa mujibu wa jarida la Forbes hadi kifo chake alikuwa anamiliki magazeti 11, vituo kadhaa vya redio na vituo kadhaa vya televisheni.Pia, ana kampuni zinazotengeneza sabuni, kampuni kubwa zaidi ya maji ya kunywa nchini. Pia, alikuwa akijihusisha na biashara ya uchimbaji madini kama ya urani, shaba na makaa. Mwaka 2014 aliwekwa nafasi ya 50 miongoni mwa watu matajiri barani Afrika, akikadaliwa kumiliki utajiri wa dola milioni 560. Kabla ya kuingia katika shughuli za kibiashara, Mengi alifanya kazi kwenye kampuni maarufu ya ukaguzi wa mahesabu ya Cooper Brothers. Mengi alisomea taaluma ya uhasibu nchini Uingereza. Mengi ameacha watoto kadhaa. | 3 |
SERIKALI imewahakikishia mazingira rafi ki wawekezaji na wadau wengine, ambao wako tayari kufanya uwekezaji nchini na kusisitiza kuwa iko tayari kushirikiana nao muda wowote.Hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde wakati wa uzinduzi wa kituo cha mafuta cha Admire kilichojengwa Kisasa. Kwa mujibu wa Msemaji wa kampuni Admire Oil Limited, Mohammed Ibrahim, kampuni hiyo imekuwa ikitoa huduma kwenye mikoa kadhaa ikiwamo Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Arusha, Pwani na Mwanza.Mavunde alisema serikali imekuwa ikithamini wawekezaji kwa sababu uwekezaji ni fursa nzuri ya ajira na mapato ya nchi kupitia kodi mbalimbali zinazolipwa.“Tuwapongeze kwa kuanzisha uwekezaji huu mkubwa katika mji mkuu, kwani kwa kufanya hivyo vijana wetu wengi watapata ajira na nafurahi kusikia kuwa kwa kufungua kituo hiki hapa tayari vijana 20 wamepata ajira,”alisema.Aidha, Mavunde alitumia fursa hiyo kuwasihi wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuja kuwekeza Dodoma. Alisema kuwa jiji hili lina fursa na wigo mpana wa maeneo ya uwekezaji, ikiwa ni pamoja na viwanda na hoteli. Awali, Ibrahim aliipongeza serikali kwa kutoka ushirikiano na kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara wanaokuja kuwekeza.Alisema kwa sasa kampuni yake imeajiri zaidi ya Watanzania 150 katika mikoa ambayo imewekeza na kuwa kati ya hao wengi wao ni wanawake, lengo likiwa ni kuboresha maisha yao. | 3 |
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara maalumu ya SMZ, Haji Omar Kheir alisema hayo wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi kwa tiketi ya CUF, Saleh Nassor Juma aliyetaka kujua lini Serikali itajenga soko la kisasa ili kuepuka wafanyabiashara wa mnada wa samaki kufanya shughuli zao katika maeneo ambayo sio rasmi.Alikiri na kusema wapo wafanyabiashara wengi wa samaki wanafanya biashara katika maeneo ya nje, ikiwemo barabarani na sio maeneo rasmi yaliyowekwa.Alisema zipo sababu nyingi zinazosababisha wafanyabiashara wa samaki kufanya kazi zao katika maeneo ambayo sio rasmi, ikiwemo ufinyu wa sehemu zilizotengwa kwa kazi hiyo.“Wafanyabiashara wetu wa samaki wanafanya kazi zao katika maeneo ambayo sio rasmi, ikiwemo barabarani na kusababisha usumbufu mkubwa na kuweka mazingira ya uchafu,” alisema.Aidha alisema baadhi ya wafanyabiashara wanakwepa kufanya kazi zao za kuuza samaki katika maeneo yaliyotengwa kwa kukwepa kutoa kodi iliyowekwa na Manispaa.Alisema kujengwa kwa soko kubwa la kisasa katika eneo la Malindi kwa kiasi kikubwa kutasaidia na kuwafanya wafayabiashara hao kutambuliwa na kulipa kodi sahihi.Kheir alisema kilichojitokeza kwa sasa ni kwamba wafanyabiashara wa samaki hulazimika kupambana na askari wa Manispaa kwa sababu ya kufanya kazi zao kinyume na sheria.Alisema ujenzi wa soko la kisasa la samaki katika eneo la Malindi unatazamiwa kugharimu jumla ya Sh bilioni 14 ambazo zitatolewa na Serikali ya Japan. | 5 |
LONDON, UINGEREZA | IDADI ya wanawake wanaowania nafasi za uongozi wakati wa uchaguzi inabadili uso wa dunia na kuchochea uwepo wa usawa wa jinsia katika mabunge ya mataifa mbalimbali. Mathalani nchi ya Mexico imechagua idadi sawa ya wanawake na wanaume bungeni katika mabunge yote mawili, hatua inayodhihirisha kuwa nchi hiyo imepiga hatua kubwa. Juni mwaka huu Serikali mpya ya Hispania, ilichaguliwa ikiwa ya kwanza tangu nchi hiyo ilipokuwa ya kidemokrasia kuwa na wanawake wengi kuliko wanaume kwenye baraza la mawaziri. Waziri Mkuu wa New Zealand, Jacinda Ardern, alijifungua mtoto wa kike Juni 21 na kuwa mwanamke wa pili pekee kuwa na mtoto akiwa madarakani, baada ya waziri mkuu, Benazir Bhutto, mwaka 1990. Hillary Clinton avutia wanawake Marekani Mwaka mmoja baada ya Hillary Clinton kushindwa nafasi ya urais nchini Marekani, kumekuwa na wanawake ambao wanawania nafasi mbalimbali nchini humo kuliko ilivyokuwa zamani. Mgombea wa chama cha Democrat, Alexandria Ocasio-Cortez, alimshinda mwanasiasa mkongwe, Joe Crowley, mwenye miaka 56, jijini New York mwezi uliopita. Binti huyo mwenye miaka 28, aliwashangaza wengi kwa kuwa hakuwa na historia ya kuwa kwenye siasa, lakini alipambana na mtu aliyetumika kwenye siasa kwa awamu 10. Profesa Farida Jalalzai, mkuu wa idara ya sayansi ya siasa katika Chuo cha Oklahoma, anaamini kuwa uthubutu wa wanawake kuwania nafasi mbalimbali ni kwa sababu pia hawapendezwi na Donald Trump. Anasema wanawake wanafanya vizuri mwaka huu kwenye bunge la Congress. Lakini kuna safari ndefu bado kwa kuwa kuna asilimia 20 pekee kwenye bunge la wawakilishi. Wanawake Bara la Ulaya wajikongoja Kwa upande wa Bara la Ulaya, wanawake wamefikia asilimia 30 kwenye mabunge ya mataifa ya Ulaya. Mwaka 2017 idadi ya wanawake iliongezeka kwenye chaguzi duniani, lakini hakukuwa na mafanikio makubwa. Ulaya ilipata wanawake wachache kuwa wawakilishi bungeni, lakini wengi walikosa nafasi hizo. Kila nchi duniani imerekodiwa kuwa na ongezeko la idadi ya wabunge wanawake tangu mwaka 1997 baada ya umoja wa mabunge (IPU) kukusanya matokeo. Miongo miwili iliyopita Sweden, Norway, Finland, Denmark na Uholanzi zilikuwa na zaidi ya asilimia 30 ya wabunge wanawake, huku Sweden ikiongoza kwa asilimia 40.4. Zeina Hilal, ambaye ni kiongozi wa masuala ya mpango wa jinsia ndani ya IPU, anasema juhudi za kufanikisha usawa kati ya wanawake na wanaume katika uwakilishi bado ndogo. “Tunasikitika kwa kuwa miaka michache iliyopita kulikuwa na ongezeko la kiasi cha asilimia 0.6 kwa mwaka 2016 na 2017, kwa miaka miwili mfululizo tumefikia uwiano wa asilimia 0.1, hii inaogofya,” anasema Hilal. IPU inakisia kuwa itachukuwa miaka 250 kufikia usawa wa jinsia kwenye mabunge. Nchi nyingi duniani hazina viongozi wanawake. Kwa sasa kuna viongozi wajuu wanawake 11 duniani, ukijumuisha marais idadi inafika 21. Kasi ya wanawake yaongezeka Angela Merkel ni kiongozi pekee aliyedumu muda mrefu kwenye Serikali ya Ujerumani tangu alipoingia madarakani mwaka 2005. Sheikh Hasina Wajed wa Bangladesh, yuko kwenye muhula wa tatu kuongoza nchi hiyo. Wanawake wengine walioingia kwenye rekodi ya uongozi ni Jacinda Ardern (New Zealand), Katrin Jakobsdottir (Iceland) na Ana Brnabic (Serbia) wote walichaguliwa mwaka 2017. Erna Solberg, alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Norway mwaka 2013. Nchini Namibia, Saara Kuugongelwa, aliingia madarakani mwaka 2015, Theresa May, akawa waziri mkuu wa pili mwanamke mwaka 2016 na Aung San Suu Kyi, akachaguliwa kuongoza nchini Myanmar. Viorica Dancila ni mwanamke wa kwanza katika historia kuwa waziri mkuu, alichaguliwa Januari mwaka 2018. Rwanda kinara wa uongozi wa jinsia Kwa mujibu wa IPU nchi za Rwanda, Cuba na Bolovia, zinaongoza kwa kuwa na wawakilishi wanawake zikiwa na zaidi ya asilimia 50. Mexico ina kiasi cha asilimia 48.6. Rwanda na nchi za Bolivia, Grenada, Mexico, Nicaragua, Costa Rica na visiwa vya Caribbean kama vile Cuba, ni miongoni mwa nchi 10 zenye zaidi ya asilimia 40 ya wabunge wanawake. Mabadiliko ya katiba mwaka 2003 ya Rwanda yameruhusu asilimia 30 ya viti kuwa vya wanawake bungeni. Tangu wakati huo wanawake wamekuwa wakijitokeza katika chaguzi mbalimbali nchini humo. Rwanda ilifanya mabadiliko hayo baada ya mauaji ya kimbari mwaka 1994 ambapo watu 800,000 wengi wanaume walipoteza maisha, wanawake walilazimika kufanya majukumu mapya mengi ili kuijenga upya nchi yao. Rwanda ni moja kati ya nchi ambazo uchumi wake unakuwa kwa kasi barani Afrika ingawa Rais Paul Kagame, amekuwa akikosolewa kuwa amekuwa akiwabana wapinzani. Baadhi ya nchi zina wanawake wachache wawakilishi bungeni, kwa mfano Yemen, Oman, Haiti, Kuwait, Lebanon na Thailand, zote zikiwa na asilimia 5 ya uwakilishi au chini ya hapo. Nchi gani hazina viongozi wanawake? Baadhi ya nchi hazina wawakilishi wanawake kabisa katika uongozi. Visiwa vya Vanuatu, Micronesia, Papua New Guinea pamoja na nchi kama El Salvador na Sierra Leone ambazo idadi ya uwakilishi wa wanawake haifahamiki. Nchini Yemen kuna mwanamke mmoja tu aliyechaguliwa bungeni kati ya wabunge 301. Mpango wa kuhakikisha kunakuwa na uwakilishi wa angalau asilimia 30 haujafanikiwa. Ufisadi ulimwangusha Shinawatra Yingluck Shinawatra, aliweka historia ya kuwa waziri mkuu wa kwanza mwanamke nchini Thailand mwaka 2011. Wakati huo alikuwa mmoja kati ya wawakilishi wanawake kwa asilimia 16 bungeni, lakini mwaka 2015 alishtakiwa kwa shutuma za ufisadi na kutoroka nchini humo. Tangu wakati huo idadi ya wanawake imeshuka mpaka kufikia asilimia 5. | 2 |
Msemaji wa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara Klabu Ya Simba Sc Haji Manara amesema kuwa timu hiyo iliharibika kipindi walipoliwa wanafundishwa na mkufunzi aliyetimuliwa Patrick Aussems Manara ametoa kauli hiyo alipokuwa akizunguma na kituo cha Wasafi Fm juu ya ujio wa kocha mpya wa klabu hiyo “Rekodi ya kufungwa mabao mengi nje ya nchi katuletea Patrick Aussems, kabla ya hapo hatukuwa hivi, hii ni kwa sababu ya mbinu zake kutobadilika awapo nyumbani na ugenini, unacheza na Al Ahly kwao unapangaje washambuliaji wawili?” Amesema Haji Aidha kwa upande mwingine Haji amemwagia sifa aliyekuwa kocha wa watani wao wa Jadi Yanga Mwinyi Zahera ambaye naye ametimuliwa “Zahera ni mwalimu ambaye anaweza kufundisha soka la kisasa kwa timu ambazo zimecheza na Yanga kwenye mechi za kimataifa Simba tungefungwa hata goli 6 kwakua Kocha Patrick Anafunguka tu hajui namna ya kubadilika kulingana na mechi husika ” ameongeza Manara Simba kwa sasa inatafuta kocha wa kudumu baada ya kumtikua Patric Aussems ambaye alifanikisha kuipeleka tiku hiyo kwenye hatua ya robo fainali ya ligi ya Mabingwa barani Afrika msimu uliopita | 4 |
Mechi itakayochezwa leo ni Njombe Mji itakayokuwa mwenyeji wa Mbao FC kwenye uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.Hatua hiyo ya nne itaendelea tena kesho kutwa kwa mechi mbili kuchezwa, ambapo Singida United itawakaribisha Polisi Tanzania, mechi ikichezwa kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.Moja ya timu zilizopanda Ligi Kuu msimu ujao, KMC itacheza na Azam kwenye uwanja wa Azam Azam Complex, Chamazi kesho kutwa saa moja usiku kabla ya mechi hiyo, Ndanda itachea na JKT Tanzania kwenye uwanja huo jioni.Aidha siku hiyo pia mabingwa wa mkoa wa Geita Buselesele FC itachuana na Mtibwa Sugar FC kwenye Uwanja wa Nyamagana, huku Majimaji FC ikicheza na mabingwa wa Ligi Kuu Bara, Yanga kwenye uwanja wa Majimaji Songea Jumatano ijayo.Hatua hii inatarajiwa kukamilika Jumatatu ijayo kwa mechi mbili, ambapo Kiluvya United itapambana na Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Mabatini, huku Stand United ikisafiri mpaka Dodoma kucheza na Dodoma FC.Akizungumzia mechi dhidi ya KMC, kocha Mkuu wa Azam FC Aristica Cioaba, amesema hataki kufanya makosa yoyote dhidi ya timu hiyo inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga, Fred Minziro.Azam Fc inaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kuvuna pointi mbili pekee katika michezo mitatu ya mwisho kwenye Ligi Kuu dhidi ya Kagera Sugar 1-1 na kutoka suluhu na Lipuli. | 4 |
Kulwa Mzee-Dar es Salaam
MAHAKAMA Kuu Kitengo cha Biashara imeiamuru Kampuni ya Kufua Umeme IPTL kuilipa Benki ya Standard Chartered Hong Kong na Benki ya Standard Chartered Malaysia Dola za Marekani 168,800,063.87.
Uamuzi huo ulitolewa na mahakama hiyo baada ya kukubali kuisajili hukumu iliyotolewa Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara Uingereza ikiitaka kampuni hiyo kulipa fedha hizo.
Jaji Baker Sehel alitoa uamuzi huo baada ya kuisajili hukumu hiyo hivi karibuni na kuamuru IPTL kulipa fedha hizo.
Alisema walalamikiwa wanaweza kuwasilisha maombi ndani ya siku 21 ya kutaka usajili huo uwekwe pambeni na taarifa ya kusajili hukumu iwasilishwe kwa walamikiwa ikionyesha haitatekelezwa mpaka zipite siku 21.
Novemba 16 mwaka jana, Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara Uingereza ilisikiliza kesi hiyo baada ya walalamikiwa kushindwa kuwasilisha utetezi wao.
Walalamikaji katika kesi hiyo walikuwa Standard Chartered Bank Hong Kong Limited na Standard Chartered Bank Malaysia wakati walalamikiwa ni IPTL, VIP Engeneering and Marketing Limited na Pan Africa Power Limited.
Katika shauri hilo walalamikiwa walishindwa kuwasilisha utetezi kwa madai kwamba mtambo wa IPTL na yote yanayohusu kampuni hiyo yako Tanzania na kwamba kabla ya kesi hiyo kuna kesi nyingine mbili nchini.
Inadaiwa msingi wa kesi hizo ni kuhusu uhalali wa Standard Chartered Bank kuwa mdai halalali wa IPTL.
Katika kesi moja, IPTL na PAP wanaidai Standard Chartered Bank Sh trilioni sita na ya pili, VIP wanaidai benki hiyo Sh trilioni moja.
Pamoja na kuwasilisha pingamizi, mahakama ilitupilia mbali na kusikiliza kesi hiyo upande mmoja. | 3 |
Asha Bani- Dar es Salaam MAMLAKA ya
Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imeanza safari mpya jana baada ya kubadilika
kutoka kuwa wakala na kuwa mamlaka kamili kisheria. Akizundua
mamlaka hiyo jana, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe,
alisema taarifa za
hali ya hewa zina umuhimu kwa shughuli za kiuchumi, ikiwemo za kilimo, uvuvi,
usafiri wa anga na majini. “TMA nawapongeza katika utendaji wao kwani
wamekuwa ni mfano wa kuigwa katika taasisi nyingine, hasa katika masuala ya
kupangilia bajeti na matumizi yake. “Katika
hili nawapongeza pia, na mkiendelea kufanya vizuri kuna haja ya kuangaliwa hata
masilahi yenu pia,” alisema Kamwelwe. Mkurugenzi
Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi, alisema Wakala wa Hali ya Hewa ambao ulifikia
ukomo wake jana, ulianzishwa mwaka 1999 kwa mujibu wa Sheria ya Wakala wa
Serikali sura 245 marejeo ya 2002. Dk. Kijazi alisema
ili kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa, Serikali imeona ni vyema
kuhuisha na kuwa mamlaka kwa lengo la kuendelea kutoa huduma bora zaidi za hali
ya hewa. Akielezea mafanikio
waliyoyapata wakiwa wakala, alisema walipata cheti cha ubora cha utoaji huduma
za hali ya hewa kwa viwango vya kimataifa katika sekta ya usafiri wa anga (ISO
9001:2008) mwaka 2011. Alisema
Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza kwa taasisi za hali ya hewa Kusini mwa Jangwa
la Sahara kupata cheti hicho. “Pia tuliendelea kuwa taasisi ya kiungo ya
kuratibu taarifa za matukio ya Tsunami nchini (National Tsunami warning
Centre). “Wataalamu
wa wakala wametoa mchango mkubwa wa kitaalamu katika Shirika la Hali ya Hewa
Dunini (WMO) na kuzisaidia baadhi ya nchi wanachama barani Afrika na nje ya
Bara la Afrika kuboresha huduma za hali ya hewa katika nchi zao,” alisema Dk.
Kijazi. Pia alisema Tanzania imeingia
katika rekodi ya dunia kwa vituo viwili, cha Bukoba na Songea kutambuliwa rasmi
kuwa na takwimu za muda mrefu za zaidi ya miaka 100. Alisema wakala umeanzishwa
mwaka 1999 na sasa wamekuwa mamlaka kamili waliokidhi mahitaji yote kisheria
kwa mujibu wa sheria namba 2 ya 2019 iliyopitishwa na Bunge na kusainiwa na
rais. “Kutokana
na uboreshaji huo, kwa sasa utabiri umekuwa ukifanyika kwa usahihi kwa asilimia
96 kutoka ile ya awali ya 87 na kufanya kazi zake kwa ufanisi mkubwa kutokana
na pia kuwepo kwa vifaa vya kisasa,” alisema Dk. Kijazi. Alisema
hata hivyo kuna vituo vya mamlaka hiyo ambavyo vinatambulika rasmi, ikiwa ni
pamoja na kilichopo Bukoba na Songea. “Vinasadia
kutoa taarifa mbalimbali ambazo pia zinatumika katika kufanya tafiti mbalimbali,
ikiwemo utabiri wa hali ya hewa, tafiti za kilimo,” alisema. Mwenyekiti
wa Bodi wa TMA, Dk. Burhan Nyenzi, alisema bodi ilifanya kazi kuhakikisha
taarifa zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa usahihi zaidi. Alisema
bodi ilikuwa na kazi ya kuhakikisha pia vituo vinaboreshwa na kuongezeka, kutoa
taarifa na kusimamia utoaji wa taarifa zake nchi nzima. | 3 |
Na EDITHA KARLO-KIGOMA WAKIMBIZI 301 kati ya 12,000 wa Burundi wanaoishi katika kambi ya wakimbizi ya Nduta wilayani Kibondo wameanza kurejeshwa kwao kwa awamu. Kurejeshwa kwa wakimbizi hao kunatokana na makubaliano baina ya pande tatu ambazo ni Serikali ya Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbuzi (UNHCR) kujiridhisha kuwa Burundi kwa sasa ina amani. Akizungumza baada ya kuwakabidhi wakimbizi hao kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi katika eneo la Mamba mpakani mwa Tanzania na Burundi, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga, alisema wanaoanza kurejea kwa siku ya kwanza ni familia 97 na awamu nyingine watawarejeshwa wiki ijayo. Alisema katika kikao wiki iliyopita cha pande zote tatu, waliamua kuanza kuwarejesha wakimbizi hao na kubainisha kuwa serikali ya Tanzania itawakabidhi kwa Serikali ya Burundi wakimbizi wa awali 301 na hadi kufikia mwishoni mwa Septemba watakuwa wamewarejesha wengine 6,000 wengine ni Oktoba na Desemba. Mkuu huyo wa mkoa aliwaomba wakimbizi hao kuanza kujitokeza kurejea mapema na wasisubiri kuondoka kwa mrundikano hali inayoweza kuwapa ugumu katika usafirishaji. Mratibu wa Wakimbizi Kanda ya Kigoma, Tony Laizer, alisema kwa sasa kuna wakimbizi 127,715 walioomba hifadhi na kati yao 12,000 wameomba kurudishwa kwao hivyo kuchelewa kuwarejesha mapema kulitokana na hali ya usalama kutokuwa nzuri baada ya kuibuka vitendo vya vurugu mara kwa mara. “Hatua hii ya kuwarejesha itasaidia kuwapo usalama na amani katika kambi kutokana na wakimbizi wengi kuomba kurejeshwa kwao… ninaamini hatua hii itasaidia kuwapa nguvu wakimbizi wengine kuendelea kuamini kuwa nchini kwao kuna amani na hatua hii itakuwa muendelezo kwa kambi zote,” alisema. Kwa upande wake,Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ya Burundi, Therence Ntahiraja alisema wao kama viongozi wa Burundi wamejipanga ipasavyo kuwapokea wakimbizi kwamba kila atakayerejea atakabidhiwa mali zake walizokuwa nazo mwanzoni na kupewa eneo ya kufanyia shughuli za kuendesha maisha. Alisema kwa sasa Burundi ina amani na kuwaomba wakimbizi wote warejee nchini kwao waweze kufanya shughuli za maendeleo na uchumi. | 2 |
Khamis Mkotya, Dar MBUNGE
wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), ametoa tafsiri pana kuhusu dhana ya
uzalendo na namna inavyopaswa kutekelezwa, ili kulinda rasilimali za taifa. Lusinde
amesema uzalendo ni hali ya kupenda kuthamini, kuheshimu rasilimali za taifa
ambao msingi wake unatokana na makuzi ya kijana, tofauti na wengi wanavyofikiri
kuwa uzalendo ni kuipenda nchi tu. Mbunge
huyo pia alisisitiza uzalendo unaovuka mipaka na kuthamini heshima, haki na
hadhi za watu, huku akiitaka jamii kujipamba na uzalendo unaovuka ubinafsi kwa
faida ya wengine. Lusinde
alitoa somo hilo juzi, wakati akiwasilisha mada katika kongamano la wasomi wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) lililofanyika Ukumbi wa Nkrumah. Kongamano
hilo lililokuwa likihusu vyombo vya habari vya Kiswahili duniani liliandaliwa
na Kigoda cha Uprofesa cha Mwalimu Nyerere katika taaluma za Kiswahili. Mbali
ya Lusinde wabunge wengine walioalikwa katika kongamano hilo lakini
hawakuhudhuria ni pamoja na Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma (CCM),
Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) na Mbunge wa Malindi, Ally Saleh (CUF). Katika
mada yake, Lusinde maarufu Kibajaji alisema ufisadi na wizi uliopo nchini hasa
serikalini umesababishwa kwa kiasi kikubwa na wasomi wengi kupungukiwa maadili
na kukosa misingi imara ya uzalendo. Aidha
mbunge huyo alitoa wito kwa bodi za kitaaluma kuanzisha kozi ya uzalendo
mashuleni na vyuoni kama hatua ya kuwaandaa vijana kuwa wazalendo. “Kwa kukosa kuzalisha wazalendo tumejikuta
tunazalisha mafisadi wengi, inabidi tuwafundishe vijana wetu uzalendo na
kuhitimu shahada za uzalendo kama mnavyozalisha wanataaluma wengine. “Kama
hamfanyi hivyo inakuwaje watu wakiwa wakubwa tunataka ghafla wawe wazalendo
kazini? Je kuna profesa yeyote hapa ambaye kawa profesa ghafla tu kwa kusema tu
awe profesa? Tunafanya makosa makubwa kwa kutaka watu wawe wazalendo ghafla
ukubwani. “Ikumbukwe
kuwa mtu anafundishwa kuwa daktari au uhandisi kwa faida ya jamii na siyo kwa
faida ya tumbo lake, lakini mtu huyo akifundishwa udaktari au uhandisi tu
pasipo kufundishwa uzalendo lazima ataishia kulisha tumbo lake na familia
yake,” alisema. Kuhusu
uzalendo unaovuka mipaka, Lusinde aliitaka jamii kuiga mifano ya wapigania
uhuru kama Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Kwame Nkrumah (Ghana) na
mwanamapinduzi Ernesto Che Guevara ambao walivuka mipaka ya nchi zao kwa
kupigania ukombozi wa bara la Afrika. “Maana
rahisi ya uzalendo imezoeleka kuwa ni kuipenda, kuona fahari ya nchi yako. Kwa
bahati mbaya wengi tunadhani ukiipenda nchi yako inabidi uzichukie nchi
nyingine, hapana huo si uzalendo,” alisema Hata
hivyo Lusinde alisema anashangaa kada ya wasomi imekumbwa na kitu gani, kwani
Rais Dk. John Magufuli, amekuwa akiwalalamikia mara kwa mara kwamba
wanamwangusha katika nafasi mbalimbali za uteuzi anazowapa. | 3 |
Kocha wa muda wa timu ya Yanga SC Boniface mkwassa amesema uwa timu hiyo itawakosa wachezaji wake muhimu wawili beki Lamine moro pamoja na straika wao mpya Tariq Seif ambaye alifunga goli pekee kwenye mchezo wao ulipita Mkwassa amesema hayo leo kwenye mkutano kueleka kwenye mechi ya watani wa wajadi inayotarajiwa kuchezwa hapo kesho kwenye uwanja wa taif jijini Dar es salaam “Tutawakosa wachezaji wawili, Lamine Moro ambaye ana kadi tatu za njano na Tariq Seif ambaye aliumia katika mechi ya mwisho lakini wengine wote wako vizuri. Kila mchezaji wetu anataka kucheza hii mechi hata kama ni leo” amesema Kwassa Kwa upande wa watani wao wa jadi naodha wa timu hiyo John Bocco amesema kuwa wao wamejoanga vizuri na hawana hofu juu ya mechi hyo licha ya kuwaheshimu wapinznai wao Yanga “Mashabiki wajitokeze kwa wingi, waweze kutuunga mkono ili tuweze kufanya vizuri, kwasababu tunaamni kama tulivyozoea timu yetu na mashabiki wetu wao ndiyo wachezaji wa 12 na tunaenda kupambana kwa ajili ya alama tatu.” amesema Bocco Ikumbukwe kuwa mchezo wa kesho unatarajiwa kuchezwa majira ya saa kumi jioni kwenye dimba la taifa jijini Dar es salaam | 4 |
HALMASHAURI mkoani Dodoma zimetakiwa kuainisha maeneo ya kuvushia na kupakia mifugo badala ya kuswaga na kupitisha kwenye miundombinu ya barabara na kusababisha uharibifu mkubwa.Akitoa ushauri huo kwenye Kikao cha Bodi ya Barabara mkoani hapa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma, Godwin Mkanwa amesema halmashauri zinatakiwa kutekelezwa matakwa ya waraka kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais kuhusu utunzaji mazingira kwa kuzingatia maeneo ya upitishaji mifugo.Mkanwa ambaye kitaaluma ni mtaalamu wa masuala ya mifugo, alisema watendaji wa halmashauri wanatakiwa kutekeleza waraka uliotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), ambazo zipo kwa kukaa pamoja na viongozi wa kata na vijiji na kuainisha maeneo ya kupitisha mifugo na sio barabarani.Amesema waraka huo unaelekeza namna mifugo inavyoweza kupita, akashauri kwamba mahali salama mifugo inaweza kupitishwa chini ya madaraja makubwa ambapo pia watembea kwa miguu wanapita kwa urahisi kuliko kupitisha barabarani na kuharibu miundombinu hiyo.Mkanwa amesema pia waraka pia unaelekeza wazi kwamba halmashauri zinatakiwa kujenga pia mahali pa kupakia mifugo ambapo ni karibu na masoko ya mifugo hiyo inapouzwa ili kusafirisha kwa urahisi kwenda Dar es Salaam na sokoni Dodoma.Akichangia Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia alisema hivi sasa umekuwa ni utamaduni kukuta makundi ya ng’ombe, punda na watoto kwenye barabara kitendo ambacho ni hatari.Akihitimisha mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge aliwataka wajumbe wa mkutano huo hasa watendaji wa halmashauri kwenda kukaa na watendaji wa kata na vijiji ili kuhakikisha mifugo wanaainisha maeneo ya kupitisha kuliko ilivyo sasa.Dk Mahenge amesema, Mkoa wa Dodoma umejaliwa kuwa na mifugo mingi, lakini ni vema utaratibu mzuri ukawekwa wa namna ya kupitisha mifugo hiyo badala ya kuswaga na kupitisha pembeni ya barabara.Awali akizungumza Mratibu wa Tanroads Mkoa wa Dodoma, Leonard Chimagu amesema wakala wake wanapambana na changamoto kubwa ya uharibifu wa miundombinu ikiwemo hiyo ya upitishaji mifugo kwenye barabara.Akisoma maazimio ya mkutano, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy alisema mkoa umeazimia kuhakikisha viongozi wa wilaya wanakaa pamoja na watendaji wa kata na vijiji ili kubainisha maeneo ya kupitisha mifugo pamoja na kuhakikisha kwamba wanaweka maeneo ya kupakilia mifugo. | 3 |
Na JANETH MUSHI -ARUSHA JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha limemkamata Mwalimu wa Shule ya Msingi
Naan, Solomon Kipuker (30), kwa tuhuma za kukutwa na bunduki ya kivita aina ya
AK47 iliyokuwa na risasi tano zilizokuwa katika magazine. Jeshi hilo pia linawashikilia
watuhumiwa wengine 12 wakiwemo watatu wanaodaiwa kuwa majangili sugu, ambao
wamekutwa na vipande vinne vya meno ya tembo ambavyo thamani yake haikuwekwa
wazi. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Jeshi la Polisi
mkoani hapa, ACP Jonathan Shanna, alisema mwalimu huyo anayefundisha katika shule
hiyo iliyopo Kata ya Enguserosambu, Tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro,
alikamatwa Juni 2, mwaka huu. Shanna alisema jeshi hilo limefanikiwa kumkamata mwalimu huyo kwa
kushirikiana na kikosi kazi kabambe dhidi ya ujangili na uhalifu wa silaha za
moto Kanda ya Ziwa chini ya uwezeshwaji wa TANAPA. Alisema mtuhumiwa huyo ni
miongoni mwa wafanyabiashara haramu wa uingizaji wa silaha za moto nchini pamoja
na biashara ya nyara za Serikali ikiwemo pembe za ndovu na faru na shughuli
nyingine za ujangili. “Mara baada ya kumhoji alikiri kumiliki silaha hiyo ya kivita
kwa kushirikiana na watuhumiwa wengine ambao bado wanatafutwa, na silaha hizo
zimekuwa zikitumika katika mapigano ya kikabila baina ya jamii za
wasonjo/watemi na wamasai na zimekuwa zikikodishwa katika matukio mbalimbali ya
ujambazi na utekaji wa watalii,wananchi na mali zao. “Hii ni mara yangu ya kwanza tangu nijiunge na Jeshi la Polisi kumkamata
mtuhumiwa ambaye ni mtumishi wa umma yuko kwenye orodha ya malipo, anapewa
mshahara halali na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akijihusisha na
matukio ya ujambazi. “Mimi nilipoambiwa na kile kikosi kabambe kwamba kimemkamata
mwalimu akiwa na silaha hii, nilidhani ni mwalimu wa ujambazi, lakini nimemhoji
kwa kina ni mwalimu halali wa shule ya msingi lakini anajihusisha na ujambazi. “Silaha hizi zimekuwa zikitafutwa kwa muda mrefu, kama
nilivyoahidi tutafanya msako wa nyumba kwa nyumba, barabara kwa barabara, uvungu
kwa uvungu, pori kwa pori ni bandika bandua mpaka kieleweke,” alisema
Kamanda Shanna. Mbali na tukio hilo, katika Kijiji cha Mbukeni, Kata ya Arash, Tarafa
ya Loliondo ilikamatwa silaha nyingine aina ya AK47 ikiwa na risasi moja imetelekezwa
katika ofisi ya kijiji hicho. Wanaodaiwa kutelekeza silaha hiyo wanaendelea kutafutwa na jeshi
hilo. Kuhusu watuhumiwa wa ujangili, Kamanda Shanna alisema Mei 30 mwaka
huu, walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao watatu (majina yamehifadhiwa), waliokutwa
katika Kitongoji cha Maji ya chai, Tarafa ya King’ori, Wilaya ya Arumeru, ambao
wanadaiwa kujihusisha na ujangili wakiwa na vipande vinne vya meno ya tembo. “Watuhumiwa hao watatu ambao tumewahoji na wamekiri kujihusisha
na biashara na ya ujangili wakiwa na vipande hivyo walivyokuwa wamehifadhi
kwenye mfuko wa sarandusi na upelelezi ili kuwabaini washirika wenzao
unaendelea,” alidai Kamanda Shanna. Katika tukio la tatu, alidai
wanawashikilia watuhumiwa watatu ambao ni Hamis Juma (37), Isiaka Islamu (22)
na Hassan Mush i(54), wakiwa na pikipiki nne ambazo hutumika katika matukio ya
wizi ambazo ni MC 978 CAH aina ya Haojue, MC 559 BHT aina ya Toyo, MC 427 BKP
na MC 789 aina ya Boxer. Alisema wanaendelea kuwahoji watuhumiwa wote na watafikishwa mahakamani
upelelezi utakapokamilika. | 3 |
KESI inayowakabili vigogo watano wa serikali akiwemo Hakimu wa Wilaya inatajwa tena leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha.Vigogo hao awali walisomewa mashitaka 11 ikiwemo uhujumu uchumi, kuteketeza ushahidi katika kesi ya ujangili ya mwaka 2017, kugushi, kutakatisha fedha haramu, kuongoza mtandao wa kufanya uhalifu, kula rushwa, kuharibu ushahidi na kuwasilisha nyaraka za uongo katika matukio waliyoyafanya katika nyakati tofauti mwaka 2016 hadi 2018.Waliofikishwa mahakamani ni pamoja na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha, Bernard Nganga (43) mkazi wa Kijenge jijini Arusha, Mwanasheria wa Serikali Fortunatus Muhalila (35) mkazi wa Lemara jijini Arusha na Wakili wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa), Maneno Mbunda (36) mkazi wa Usa River wilayani Arumeru mkoani Arusha.Wengine waliofikishwa katika Mahakama hiyo ni pamoja na mtuhumiwa wa ujangili Kanda ya Kaskazini, Nelson Kangero (62) mfanyabiashara mkazi wa Mwanga mkoani Kilimanjaro na mshirika wake, Tumaini Mdee (40), mfanyabiashara mkazi wa Njiro Kata ya Engutoto jijini hapa.Waendesha Mashitaka wa Serikali, Javelin Rugahiruzwa, Shedrack Kimaro na Theophil Mutakyawa waliwasomea washitakiwa hao mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Arusha, Niku Mwakatobe na hawakutakiwa kujibu chochote kwa kwa mahakama hiyo haina uwezo wa kisheria kusikiliza kesi hiyo.Rugahiruzwa aliieleza Mahakama hiyo kuwa shitaka la kwanza linamkabili mshitakiwa wa kwanza Kangero na mshitakiwa wa tano Mdee kwa kuongoza mtandao wa uhalifu kwani ilidaiwa kuwa Juni Mosi mwaka 2018 na Aprili 15, mwaka huu kwa nyakati tofauti ndani ya Jiji la Arusha na Mkoa kwa ujumla, walishirikiana na watumishi wa umma kutoa rushwa.Alisema shitaka la tatu linawakabili mshitakiwa wa pili Wakili Mbunda na mshitakiwa wa tatu Hakimu Nganga na mshitakiwa wanne Mwanasheria wa Serikali Muhalila ambao wote kwa pamoja wanashitakiwa kwa kuongoza mtandao wa rushwa kwani ilidaiwa kuwa kati ya Juni Mosi mwaka 2018 na Aprili 15, mwaka huu, wakiwa watumishi wa umma kwa makusudi walipokea rushwa kwa lengo la kutenda uovu wakati wakijua wazi kufanya hivyo ni kinyume cha sheria. | 3 |
Kiongera amerudishwa Simba kwenye dirisha dogo la usajili mwishoni mwa mwaka jana akitokea KCB ya kwao Keny alipokuwa akicheza kwa mkopo, lakini ameshindwa kuonesha kiwango cha kuridhisha na kuishia kukaa benchi.“Nimeanza vibaya kwa sababu nimekuta wachezaji wengi wapo fiti na ushindani wa nafasi ya kucheza ni mkubwa tofauti na ilivyokuwa msimu uliopita ambao niliumia. “Lakini nimechukua kama changamoto nitahakikisha najipanga kufanya mazoezi ya nguvu zaidi ili kumshawishi kocha aweze kunitumia kikosi cha kwanza,” alisema Kiongera.Mshambuliaji huyo aliyewahi kutamba na Gor Mahia ya Kenya, alisema anajua mashabiki wa timu yake wana matumaini makubwa kutoka kwake kutokana na kiwango alichokuwa nacho kabla hajaumia msimu uliopita na kuwataka mashabiki kuendelea kumsapoti.Alisema hali kama hiyo ni ya kawaida kwa mchezaji kutokea, lakini atahakikisha anaongeza muda wa mazoezi ili kurudi kwenye kiwango chake kilichozoeleka kwa mashabiki wa timu hiyo na kuisaidia Simba kufikia malengo iliyojipangia. Tangu arejee Simba, Kiongera amecheza mechi mbili za Ligi Kuu dhidi ya Toto African na Mwadui FC. | 4 |
JESHI la Polisi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora limefanikiwa kumkamata na kumfi kisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Igunga, Nyalagi Saimon (30), mkazi wa kitongoji cha Mwanzugi kwa tuhuma ya kumchoma moto mwanawe.Awali Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Wilaya ya Igunga, Elimajid Kweyamba aliiambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi wa wilaya hiyo, Lydia Ilunda kuwa mshitakiwa Nyalagi Saimon alitenda kosa hilo Machi 17, mwaka huu.Kweyamba alisema katika tarehe hiyo majira ya saa tatu usiku mtaa wa Fisi, mshitakiwa akiwa mwangalizi na baba wa mtoto huyo ambaye jina lake limehifadhiwa alimfanyia vitendo vya ukatili kwa kutumia upanga alilokuwa ameliweka kwenye moto.Alisema mshitakiwa alikuwa akiutoa upanga kwenye moto kisha kumchoma nao kwenye miguu yote miwili, jambo ambalo ni kosa na ni kinyume na kifungu 169 A kanuni ya adhabu sura ya ya 16.Hata hivyo, baada ya kusomewa mashitaka hayo, Simon alikana kutenda kosa hilo na kesi hiyo imeahirishwa na itatajwa tena Aprili 12, mwaka huu na mshtakiwa alirudishwa mahabusu.Wakati huo huo, mkazi wa kijiji cha Mwabalatulu wilayani Igunga mkoani hapa, Sagwa Shigela (35) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Igunga kwa tuhuma ya kumnajisi mtoto wake wa kumzaa wa miaka 13.Mwendesha Mashitaka wa Polisi Wilaya ya Igunga, Elimajid Kweyamba aliiambia Mahakama mbele ya Hakimu wa Wilaya ya Igunga, Lydia Ilunda kuwa mshitakiwa Sagwa Shigela alitenda kosa hilo kati ya Januari 13 na 14 mwaka huu.Kweyamba alisema katika tarehe hizo mshitakiwa Shigela kwa makusudi akiwa baba mzazi wa mtoto huyo wa miaka 13 alimnajisi, tendo ambalo kosa na ni kinyume na kifungu 158(1) (a)(2) kanuni ya adhabu sura ya 16 mapitio ya mwaka 2002 inayozuia kutenda makosa kama hayo.Baada ya mshitakiwa kusomewa mashitaka hayo, alikana kosa hilo na mshtakiwa alirudishwa mahabusu na kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na itatajwa tena Aprili 14, mwaka huu. | 3 |
ZURICH, USWISI
MKURUGENZI wa Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Walter De Gregorio, amefutwa kazi baada ya kutoa maneno yenye utani kuhusu shirikisho hilo kwenye televisheni ya Uswisi.
Gregorio alizungumza kwenye kipindi cha Schawinski kuwa: “Rais wa Fifa, Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa Mawasiliano wote wanasafiri kwenye gari. Nani ni dereva? Jibu ni polisi.”
Fifa imetangaza jana kwenye taarifa yao kuwa De Gregorio ameamua “kuachia madaraka kwenye ofisi yake”.
Lakini inaaminika ya kuwa aliambiwa ajiuzulu na Rais wa Fifa, Sepp Blatter na katika taarifa hiyo imeeleza kuwa De Gregorio atabakia Fifa kama mshauri hadi mwishoni mwa mwaka huu.
Blatter yeye alitangaza ataachia ngazi kuongoza taasisi hiyo mwanzoni mwa mwezi huu kutokana na kashfa kubwa ya rushwa inayoiandama Fifa na sasa uchaguzi mwingine utafanyika kati ya Desemba na Februari mwakani.
De Gregorio, 50, amedumu kwenye wadhifa huo tangu Septemba, 2011 na amekuwa mtu wa karibu sana wa Blatter tangu achukue majukumu hayo na inaelezwa Blatter hakufurahishwa na maneno yake hayo. | 4 |
MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) imesema hifadhi hiyo inakabiliwa na ongezeko kubwa la fi si inayofi kia 600 kutoka 200 waliopo, idadi ambayo ni kubwa na imekuwa ikisababisha madhara kwa wanyama na tishio kwa binadamu.Akizungumza jijini hapa, Kamishna wa hifadhi hiyo, Dk Fredy Manongi alisema baadhi ya wanyama walioathirika na ongezeko la fisi ni pamoja na duma ambao watoto wao huwa wanaliwa na fisi na kutishia kutoweka kwa wanyama hao ambao wamekuwa wakiwindwa na makundi makubwa ya fisi wenye njaa kali.Alisema hivi sasa mamlaka hiyo inatekeleza mradi wa kudhibiti fisi ndani ya hifadhi hiyo, wakiona inafaa baada ya utafiti wa mradi huo watapunguza fisi hao ili kuwezesha hifadhi hiyo kuwa na fisi wachache kulingana na eneo la hifadhi hiyo. Kuhusu idadi ya simba, Kamishna Manongi alisema ndani ya hifadhi hiyo kuna simba wapatao 1,172 ambao idadi yao haiongezeki kwa kiwango kikubwa.Akizungumzia ujenzi wa mradi wa jengo la ghorofa 14 ambalo ni kitega uchumi cha mamlaka hiyo, alisema ni mradi mbadala wa kuiwezesha mamlaka hiyo kupata kitega uchumi kingine iwapo hifadhi itatetereka kutokana na mtikisiko wa uchumi duniani pindi ukitokea tena na kuathiri sekta hiyo ya utalii.Alisema gharama za awali za mradi huo ilikuwa ni Sh bilioni 42 kutokana na mabadiliko yaliyotokana na kupanda kwa bei ya gharama za vifaa vya ujenzi, gharama hiyo iliongezeka hadi kufikia Sh bilioni 45 na hadi sasa jumla ya Sh bilioni 39.4 zimeshalipwa kwa mkandarasi wa jengo hilo.Akizungumzia mradi wa jengo hilo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantine Kanyasu ameiagiza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) kulitangaza jengo lake la kitega uchumi lenye urefu wa zaidi ya ghorofa 10 lililopo katikati ya Jiji la Arusha ili liweze kupata wawekezaji, hivyo kuingizia mapato mamlaka hiyo . | 3 |
MFANYAKAZI wa Kampuni ya Ulinzi ya Security Guard Paul John (raia wa Malawi) (30) ameburuzwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, kwa tuhuma za kunajisi mtoto wa miaka saba.Pamoja na shauri hilo, pia watuhumiwa wawili ambao ni Shukuru Hassan (38) na Said Shabani (34), wamepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka kwa tuhuma ya kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha.Katika kesi ya kwanza ya kunajisi, Mwendesha Mashtaka Hellen alidai mbele ya Hakimu Ester Mwakalinga kuwa John alitenda kosa hilo Machi 25, mwaka huu katika eneo la tegeta Nyuki wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.Hata hivyo, mtuhumiwa alikana kutenda kosa hilo na kesi hiyo iliyoahirishwa hadi Septemba 10, mwaka huu.Mtuhumiwa alirejeshwa mahabusu baada ya kushindwa kukidhi masharti ya dhamana ambayo ni kuwa na wadhamini wawili ambao ni watanzania, kuwa na wafanyakazi kutoka taasisi zinazotambulika na serikali wakiwa na vitambulisho na barua za utambulisho kutoka kwenye ofisi zao.Katika kesi nyingine Hassan na Shaban wamesomewa mashtaka ya tuhuma za unyang’anyi wa kutumiwa silaha.Mwendesha Mashtaka, Yusuph Aboud alisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Frank Mushi, ambapo alidai kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa hilo, Novemba 14, mwaka 14, mwaka jana.Alidai kuwa washtakiwa hao walipora vitu mbalimbali kama vile kompyuta 12, UPS DDR, Printa moja, na vingine vyenye thamani ya Sh milioni milioni 48.9 ambavyo ni mali ya kampuni ya City Mortagage na Finance Ltd. | 3 |
Na Justin Damian, Baada ya mvutano wa muda mrefu kati ya Serikali na makampuni ya simu, hatimaye Vodacom Tanzania imekuwa kampuni ya kwanza ya simu kupiga hatua moja katika utaratibu wa kujiunga na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), kwa kutangaza nia ya kuuza hisa zake za kwanza (IPO). Katika hatua hiyo ya kwanza, Vodacom Tanzania imepeleka maombi ya muundo na muda wa kujiorodhesha DSE kwa Mamlaka ya Dhamana na Soko la Mitaji (CMSA). Mamlaka hiyo itapitia maombi hayo kuona kama inakidhi vigezo vya kisheria kabla ya kuiruhusu kuendelea mbele. Baada ya kujiunga na DSE, Vodacom itajulikana kama Vodacom Tanzania Public Limited Company (Plc). Kujiorodhesha kwa Vodocom katika soko la hisa, kuna maana kwamba sasa wananchi wa kawaida wataweza kumiliki kampuni hii ambayo imekuwa ikitengeneza faida ‘nono’ kila mwaka. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Vodocom Tanzania ndiyo kampuni kubwa zaidi katika soko la huduma za mawasiliano kwa simu za kiganjani kati ya kampuni saba, ikichukua asilimia 31 ya soko na laini milioni 12.06 hadi kufikia Juni mwaka huu. Kampuni za Tigo na Airtel zinashikilia nafasi ya pili na ya tatu kwa kuwa na asilimia 29 na 26 ya soko. Kampuni ya Tigo ina laini milioni 11.6, huku kampuni ya Airtel ikiwa na laini milioni 10.3. Vodacom imekuwa kampuni ya kwanza ya simu kujiorodhesha DSE wakati ukiwa umebaki mwezi mmoja tu kwa makampuni mengine kujiorodhesha, ikiwa ni agizo la Serikali kutaka makampuni yote kujisajili DSE kufikia 1/01/2017. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa Watanzania wananufaika na biashara hii yenye faida kubwa na kuhakikisha nchi inanufaika zaidi na sekta hii inayokuwa kwa kasi kubwa. Hatua ya kampuni za simu kujisajili DSE itaongeza uwazi wa namna makampuni hayo yanavyoendeshwa na pia itakuwa rahisi kulipa kodi zote zinazostahili kwa Serikali. Itakumbukwa kuwa kwa miaka kadhaa, Kampuni ya simu ya Vodacom imekuwa kinara katika ulipaji kodi na hatua hii ya kujisajili DSE, kunaweza kusaidia kuongezeka kwa kiasi ilicholipa serikalini kama kodi. Hatua ya makampuni ya simu kujiorodhesha DSE si geni ila limecheleweshwa kwa njia moja au nyingine kwani ni utekelezaji wa sheria ya Elektroniki na Mawasiliano ya Posta (EPOCA) na Sheria ya Fedha ya mwaka 2016 inayoelekeza makampuni ya simu kumilikishwa asilimia 25 ya hisa zake kwa wananchi kwa kujiunga na DSE. Mafanikio haya yanakuja baada ya msuguano mkali na wa miaka mingi kati ya Serikali na makampuni haya ambayo mengi ni makubwa na ya kigeni kwa kuwa wakati mwingine sheria zao hukinzana na za kwetu na hivyo kuhitaji utangamano wa kisheria. Chama cha Wenye Makampuni ya Simu Tanzania (MOAT) kilikuwa kikipinga vikali hatua hii kwa madai kuwa ni kinyume na sheria mbalimbali ikiwamo Sheria ya Makampuni, Sheria ya Soko la Mitaji na hata Katiba ya nchi kwenye kipengele cha umiliki wa mali binafsi. Mengi yalitokea wakati wa mchakato wa muswada wa kuyataka makampuni ya simu kujiunga na DSE kama sharti la leseni. Mwenyekiti wa Bodi ya DSE, Peter Mchunde, alijiuzulu nafasi yake kwa kile kilichodaiwa kupinga Muswada huo ambao hata hivyo Rais Jakaya Kikwete aliusaini kuwa Sheria. Mchunde alimwandikia Rais Kikwete na kumweleza kuwa, kuyalazimisha makampuni ya simu kujiunga na DSE kungeyafanya makampuni yenye nia ya kuwekeza kwenye sekta ya mawasiliano ya simu kukata tamaa na kuachana na mpango wa kuwekeza kwenye sekta hii. Wachunguzi wa mambo wanasema kama sababu ndiyo hiyo, Mchunde alionesha udhaifu mkubwa wa uzalendo na uongozi kwani ni wazi wenye kampuni wao hufuata faida popote ilipo na si mapenzi au kuburuza nchi. Kwao kila kitu ni fursa. Hata hivyo, hofu ya makampuni ya simu kujiunga na DSE inatokana na hofu ya kupungua kwa kiwango cha faida wanachokipata kutokana kuwa mara tu watakapojisajili na watu kununua hisa, watatakiwa kuweka wazi hesabu zao za fedha na gharama zao nyingine za uendeshaji kwani wanawajibika na sheria ya mitaji kufanya hivyo. Itakumbukwa kuwa hatua ya Muswada ilipokelewa vizuri na Chama cha Madalali ambao walisema makampuni ya simu yalikuwa yakihofia kujisajili DSE kwa kuogopa kuweka wazi taarifa zao za kifedha. Pamoja na kwamba Vodacom imekuwa kinara wa kulipa kodi miongoni mwa makampuni ya simu, haijawahi kuweka wazi hesabu zake na kuonyesha kwa mfano mapato yake kwa mwaka ni shilingi ngapi pamoja na matumizi yake. Ukitaka kupata itabidi uulize Uingereza au Afrika Kusini ambako imesajiliwa. Makampuni mengi yamekuwa yakijificha nyuma ya sheria ya kodi ya Tanzania ambayo inasema kiasi anacholipa mtu au kampuni ni siri yake ambayo haiwezi kutolewa kwa umma, labda kama taarifa hizo zitahitajika na vyombo vya sheria. Hatua hii ya kuyalazimisha makampuni ya simu ambayo yanatengeneza faida kubwa itasaidia sana katika kuweka uwazi katika uendeshaji wa makampuni haya ambapo pia Watanzania wataweza kuyamiliki kwa dhana nzima ya kuwa na hisa na kuvuna faida. Serikali kwa upande wake pia itaweza kupata mapato zaidi kwa kuwa kila kitu kitakuwa wazi. Kimsingi faida ya kampuni hizo zinalingana na modeli ya uchumi wa mafuta na gesi na hivyo huwa ni fedha nyingi sana, ingawa bei ya mauzo kiwango chake ni kidogo. Kadiri kampuni ikiwa na wateja wengi ndivyo inavyotengeneza faida. Mamlaka ya Hisa na Mitaji (CMSA) itayapitia maombi hayo ya Vodacom, ikitazama kwa undani namna inavyoweza kutekeleza utoaji taarifa na hatari za utendaji kabla ya kuorodheshwa kwenye soko la DSE na aina ya ushiriki wake sokoni. “Tunafurahi kuutangazia umma kuwa tumeleta maombi yetu rasmi ya Kujiunga na nia ya kutekeleza mahitaji ya Sheria na muundo na ratiba kamili ya kujiunga kama muhtasari wa nia ya Kampuni yetu unavyosema,” anasema Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Ian Ferrao. Hii ni kampuni ya kwanza, nyingine ni Airtel, Tigo, Halotel, TTCL, Smart na Zantel. Serikali ilishatangaza TTCL ambayo inaimiliki kwa asilimia 100 itaingia soko la hisa mwakani na Airtel ambayo ina asilimia 40 ya umiliki inajipanga, wakati Halotel ndio kwanza imeingia sokoni na huenda ikasubiri hadi miaka mitatu ipite kama sheria inavyoruhusu na hakuna kauli kutoka Smart. Kuhusu Zantel, asilimia 15 ya hisa ni mali ya Serikali ya Zanzibar na ilisajiliwa kule. | 3 |
Yanga inahitaji pointi tatu kutwaa ubingwa huo kwani itafikisha pointi 55 ambazo hazitafikiwa na timu yoyote. Azam inayoshika nafasi ya pili ikiwa na pointi 45 itafikisha pointi 54 endapo itashinda mechi zake tatu zilizosalia.Ingawa kwenye mpira lolote linaweza kutokea, lakini kwa mwenendo wa matokeo inayopata Yanga katika mechi zilizopita, ni wazi Polisi ina kazi kubwa kuizuia leo.Yanga iliifunga Ruvu Shooting mabao 5-0 katika mechi iliyopita wakati Polisi ililazimishwa sare ya bila kufungana na Coastal Union. Katibu Mkuu wa Yanga Dk Jonas Tiboroha alisema jana kuwa uongozi tayari umeanza maandalizi kusherehekea ubingwa kwa mtindo wa aina yake.“Uongozi wa Yanga unapenda kuwaalika wanachi wa Tanzania na nchi jirani kuungana nasi kesho (leo) katika shamra shamra za ushindi wa ubingwa wa michuano ya Ligi Kuu nchini,” ilisomeka sehemu ya taarifa ya Dk Tiboroha kwa waandishi wa habari.“Sisi kama Yanga tumejipanga kwa staili ya tofauti kabisa katika kuuchukua ubingwa wa Ligi Kuu,” alisema. Akizungumzia mechi ya leo kocha wa timu hiyo, Hans van der Pluijm alisema anatarajia kufika safari ya ubingwa salama leo.“Tuna matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo wa kesho (leo) na huo ndio tunaotegemea kutangaza ubingwa,” alisema.Alisema si kwamba atapata ushindi kirahisi bali amewaandaa wachezaji wake vizuri na anaamini watafanya alivyowaelekeza ili kuibukia na ushindi na kutangaza ubingwa mapema.Yanga watasafiri kwenye Tunisia kucheza mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho na Etoile de Sahel ya huko itakayochezwa mwishoni mwa wiki hii | 4 |
SERIKALI imesema hadi Agosti, mwaka huu, Mkandarasi wa Kuendesha Mradi wa Usafi ri wa Ma-basi Yaendayo Haraka Dar es Salaam, atakuwa amepatikana kuendesha mradi huo.Akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, Tamisemi na Utumishi na Utawala Bora, Naibu Waziri-Tamisemi, Josephat Kandege alisema lengo la serikali ni kuhakikisha mwezi huu inatangaza zabuni. Alisema ni azma ya serikali kuhakikisha msongamano Dar es Salaam unapungua ndiyo maana inajenga miundombinu na kuboresha ili kuhakikisha kunakuwa na usafiri bora zaidi.Alisema kwa sasa usafiri huo unasimamiwa na mwendeshaji wa muda, lakini mwendeshaji mpya akipatikana magari yataongezeka kutoka 140 ya sasa hadi 305 kwa ajili ya kuboresha usafiri katika jiji hilo muhimu kibiashara. Alisema kuboresha usafiri jijini Dar es Salaam, serikali itaendelea kujenga barabara kutoka katikati ya jiji kwenda pembezoni kupitia barabara ya Kilwa na kwenda Gongo la Mboto. “Vile vile itaendelea na ujenzi wa barabara kutoka Jijini hadi Tegeta ili kuhakikisha usafiri unaimarika jijini Dar es Salaam,” alisema.Akichangia kuhusu Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (Tarura), Kandege alisema wabunge wamesifia utendaji wake lakini wakaomba iimarishwe ili kuondoa upungufu unaojitokeza. Alisema ni kweli kilometa zinazohudumiwa na Tarura ni nyingi na mgawanyo wa fedha za ujenzi wa barabara ni kidogo, lakini kulikuwa na sababu mbalimbali za kufikia fomula hiyo.Kupitia utendaji huo, serikali imeunda Tume kutathmini kupitia upya fomula ya mgawanyo wa fedha za kujenga miundombinu baina ya Tarura na Wakala wa Barabara (Tanroads). Alisema fomula ya sasa inaonesha Tarura wanapata asilimia 30 na Tanroads asilimia 70 wakati Tarura ina mtandao mrefu zaidi.Naibu Waziri Tamisemi, Mwita Waitara alisema, serikali imejitahidi katika elimu kwa shule za msingi bure ambapo bajeti imekua kutoka Sh bilioni 249 hadi Sh bilioni 288. Alisema kuongeza bajeti kunalenga watoto wa umri kusoma wanapata elimu ya msingi bure. Kuhusu hoja ya watendaji ngazi za mitaa na vijiji wanaokaimu, Mwita alisema halmashauri zinatakiwa kupeleka orodha ili wanaokaimu wathibitishwe kazini kufanya kazi kwa umakini. | 3 |
TEHRAN, IRAN RAIS wa Iran, Hassan Rouhani ameonya vikosi vya nje vinatishia usalama wa
eneo la Ghuba, baada ya Marekani kudai inatuma wanajeshi eneo hilo. Rais Rouhani, alisema vikosi vya nje siku zote
vimesababisha ‘uchungu na masikitiko’ na havipaswi kutumika katika ‘ushindaji
wa silaha’. Marekani inatuma wanajeshi zaidi Saudi Arabia,
baada ya shambulio dhidi ya vituo vyake vya mafuta, hatua ambayo mataifa yote
mawili yanaishutumu Iran kutekeleza. Alisema Iran itawasilisha mpango mpya wa amani wa
Ghuba kwa Umoja wa Mataifa siku zijazo. Mwaka huu, kumeendelea kushuhudiwa uhasama baina
ya Marekani na Iran, kutokana na hatua ya Rais Donald Trump kujitoa katika
makubaliano ya nyuklia yalionuiwa kudhibiti shughli za Iran za nyuklia ili kwa
upande wake ipunguziwe vikwazo. Hatua ya hivi karibuni hali iliyozusha joto,
inatokana na mashambulio ya makombora na ndege zisizokuwa na rubani dhidi ya
vituo vya mafuta vya Saudi Arabia huko Abqaiq na Khurais Septemba 14, mwaka huu. Waasi wa Houthi nchini Yemen, wanaoungwa mkono na
Iran walisema wao ndio waliotekeleza shambulio hilo, lakini Marekani na Saudia
zinasema Iran ndiyo iliohusika. Alikuwa akizungumza katika kumbukumbu ya kuanza
kwa vita vya Iran – Iraq vya mnamo 1980-1988
na maonyesho ya kijeshi yaliokuwa yakifayika mjini Tehran na katika miji
mingine. “Vikosi vya nje vinnaweza kuzusha matatizo
na ukosefu wa usalama kwa watu wetu na eneo letu,” alisema katika hotuba
ya taifa iliyorushwa na luninga. Ametaja kutumwa kwa vikosi hivyo katika siku za
nyuma kama janga na amewaambia wanajeshi hao ‘wakae mbali’. “Kwa ni wakweli, basi wasilifanye eneo leu
kuwa ni sehemu ya ushindani wa silaha… munavyozidi kukaa mbali na maeneo na
mataifa yetu ndipo kunapozidi kuwa na usalama zaidi.” Vipi kuhusu mpango wake wa amani? Rais huyo amesema mpango huo wa amani
utawasilishwa kwa Umoja wa mataifa, unaoanza vikao vya baraza kuu mjini New
York Ijumanne. Hatahivyo, hakutoa taarifa akisema tu kwamba
amani katika mfereji wa Hormuz inaweza kufikiwa “kwa ushirikiano wa
mataifa tofauti”. Rouhani amesema Iran “ipo tayari kuachana na
makosa ya zamani” yaliotekelezwa na majirani wa kieneo. “Katika wakati huu muhimu wa kihistoria
tunawatangazia majirani zetu kwamba tunanyoosha mkono wa urafiki na undugu
kwao,” amesema. Waasi wa Houthi nchini Yemen pia wamependekeza
mpango wa amani wakisema watasitisha mashambulio yote dhidi ya Saudi Arabia ili
muradi ufalme huo na washirika wake wafanye vivyo hivyo. Mjumbe maalum wa Marekani nchini Yemen Martin
Griffiths amesema katika taarifa ni muhimu “kuitumia fursa hii na kusogea
mbele kwa hatua zote kupunguza ghasia, hatua za kijeshi na majibizano
yasiosaidia”. Nini maaa ya kutumwa vikosi vya Marekani? Wizara ya ulinzi Marekani ilitangaza Ijumaa
kufuatia ombi la Saudia , kwamba watatumwa wanajeshi wa kiasi fulani katika
ufalme huo, sio maelfu na watakaoshughulika na mfumo wa ulinzi wa angani na wa
makombora. Waziri wa ulinzi Mark Esper amesema:
“Tutashirikiana kushinikiza kuwasilishwa kwa vifaa vya kijeshi.” Tangazo hilo limechangia muitikio mkali kutoka
kwa jeshi la Iran Revolutionary Guard IRGC – kitengo cha juu cha jeshi Tehran
kilichotambuliwa na Marekani kama kundi la kigaidi. Kamanda meja Jenerali Hossein Salami amesema:
“Yoyote anayetaka ardhi yao kugeuka eneo la mapambano, endelea. Jihadhari,
uchokozi mdogo hautosalia kuwa mdogo. Tutamuandama mchokozi yoyote.” | 2 |
Kulwa Mzee, Dar es Salaam Aliyekuwa
Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Mrakibu wa Polisi (SP), Christopher
Bageni, aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kuwaua wafanyabiashara wa madini kutoka
Mahenge mkoani Morogoro, amepinga adhabu hiyo katika Mahakama Rufaa jijini Dar
es Salaam. SP
Bageni amewasilisha maombi ya mapitio Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ambayo
yamepangwa kusikikizwa Juni 16, mwaka huu mbele ya jopo la majaji watatu,
Stellah Mugasha, Ferdinand Wambali na Rehema Kerefu. Katika maombi yake ya mapitio, Bageni amewasilisha sababu mbalimbali za kupinga adhabu hiyo ikiwamo kwamba jopo la majaji lilifanya makosa ya dhahiri katika muonekano na hivyo kusababisha haki kutozingatiwa katika kutoa hukumu hiyo. SP Bageni alihukumiwa adhabu hiyo Septemba 16 mwaka 2016 na Mahakama ya Rufaa ya Tanzania mbele ya jopo la majaji watatu, Jaji Benard Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage. Mahakama
ya Rufaa ilitoa hukumu hiyo baada ya kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi
wa Mashtaka nchini (DPP) akipinga aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es
Salaam (RCO) Kamishna Msaidizi wa Polisi, Abdallah Zombe na maofisa wenzake
watatu akiwemo Bageni kuachiwa huru na Mahakama Kuu mwaka 2009. Hukumu
hiyo ilisomwa na aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufaa wakati huo, Jaji
John Kahyoza. Aliwataja wajibu rufani kuwa ni Zombe, SP Bageni, aliyekuwa Mkuu
wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP)
Ahmed Makelle na Rajabu Bakari. Katika
kesi hiyo, wafanyabiashara wa madini waliouwawa ni Sabinus Chigumbi, maarufu
Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva taksi, mkazi
wa Manzese Dar es Salaam, Juma Ndugu. Walidaiwa
kutenda makosa hayo Januari 14, mwaka 2006, katika Msitu wa Pande, uliopo
wilayani Kinondoni baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao Sinza, walipokuja
Dar es Salaam kuuza madini. | 3 |
Kangoye alisema hayo jana baada ya kufungua duka la Tigo, lililokarabatiwa na kampuni hiyo, kwa lengo la kutanua wigo wa huduma zake kwa wananchi wa Jiji la Arusha ambapo hapo awali walikuwa wakitumia muda mrefu kupata huduma hiyo.Alisema kazi ya kuleta maendeleo ni ya kila Mtanzania na sekta binafsi na taasisi zingine.Mkuu huyo alisema pamoja na kwamba kampuni za simu zinafanya jitihada kubwa kuisadia serikali, lakini kasi yao inapaswa kuongezeka tena maradufu.Akizungumzia kampuni ya Tigo, Mkuu huyo alisema na kuutaka uongozi wa kampuni hiyo kufanya kila linalowezekana kuhakikisha inaboresha na kuongeza huduma zake na kuwa bora ulitukuka kwani wananchi wanahitaji huduma bora na sio bora huduma.Kangoye alisema kuwa huduma ya Tigo-Kilimo iliyoanzishwa na kampuni hiyo ni muhimu sana kwa kila mtanzania, kwani itamsaidia mkulima kujua bei ya mazao na kipindi gani mkulima anapaswa kuandaa kilimo chake kwa kupata taarifa rasmi katika simu ya kiganjani ya mtandao wa Tigo.Meneja ubora wa huduma kwa wateja wa Tigo, Mwangaza Matotola alisema kuwa ukarabati wa duka hilo ni mojawapo ya mikakati ya Kampuni ya Tigo ya kutanua wigo wa huduma zake kwa wananchi.Matotola alisema duka hilo, Tigo litahudumia watu zaidi ya 300 kwa siku na kuwapatia huduma mbalimbali, kama intaneti Mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini, David Charles alisema kufunguliwa kwa tawi hilo kutawasaidia wakazi wa Arusha kutotumia muda mwingi barabarani kutafuta huduma ya kampuni hiyo. | 5 |
Na ELIUD NGONDO- SONGWE BAADHI ya wafanyabiashara wilayani Ileje mkoani Songwe, wameiomba Serikali kutengeneza miundombinu mizuri ya kufanyia biashara katika mpaka wa Isongole ambao unatenganisha nchi za Tanzania na Malawi. Hayo yamesemwa jana na baadhi ya wafanyabiashara wanaofanyia shughuli zao katika daraja la Mto Songwe ambao ndio mpaka wa nchi hizo mbili za Tanzania na Malawi. Mmoja wa wafanyabiashara hao, Andakson Kamendu, alisema wao wamekuwa wakifanya biashara zao katika eneo hilo mpaka ambapo kuna daraja la Mto Songwe, hivyo miundombinu iliyopo si rafiki kwa shughuli hizo. Alisema Serikali kuu imeanza kutekeleza ujenzi wa barabara ya kutoka Mpemba hadi Isongole kwa kiwango cha lami, hivyo kukamilika kwake itakuwa ni fursa ya kuongeza uchumi kwa wananchi. Alisema wamekuwa wakiuza bidhaa zao mpakani hapo wakiwa wamekaa juani kutokana na kutokuwepo kwa miundombinu ambayo ingewawezesha kufanya biashara hizo kiurahisi. Naye Elia Mwampashi, alisema mpaka huo ukiwekewa miundombinu mizuri unaweza kuwa chanzo kikubwa cha kuongeza mapato kwa Serikali ya Tanzania kutokana na nchi nyingi kupitishia mizigo hapo. Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Joseph Mkude, alisema Serikali ipo katika mkakati wa kutengeneza barabara ya Isongole hadi Mpemba kwa kiwango cha lami. Alisema wakandarasi wapo katika hatua ya kujenga makambi ambayo yatatumika wakati wa utengenezaji wa barabara hiyo, hivyo miundombinu ya kibiashara ikiwekwa vizuri itakuwa ni fusa ya kuongeza uchumi. | 3 |
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya, alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele. “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema | 5 |
WELLINGTON, New Zeiland WAZIRI anayeshughulikia masuala ya wanawake nchini hapa amelazimika kuendesha baiskeli kwenda hospitali kwa wiki 42 kwa ajili ya kujiandaa kujifungua mtoto wake wa kwanza kwa kile ambacho anadai hawakuwa na nafasi ya kutosha ndani ya gari lao na mumewe kwa ajili ya watoa huduma. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Waziri huyo kutoka chama cha Green, Julie Genter, alisema mbali na kukosekana nafasi katika gari hilo, alilazimika kutumia usafiri huo ikiwa ni sehemu ya mazoezi ya kijiweka vizuri katika nafya. Kupitia ujumbe na picha ambazo azilizutuma jana katika mtandao wake wa jamii wa Instagram aliandika kwamba yeye na mumewe walikuwa wanaifurahia asubuhi hiyo njema. “Kitu hiki ndicho kinachotupa bahati,” aliwaandikia wafuasi wake kupitia mtandao huo wa jamii. “Mimi na mume wangu tulipanda baiskeli kwa sababu hapakuwa na nafasi ya kutosha katika gari kwa ajili ya wafanyakazi wa msaada … lakini pia iliniweka mimi katika hali nzuri zaidi. “Safari ya kutumia baiskeli ya umeme ilikuwa ni nzuri kwa kiasi kikubwa naifurahi safari hii na tunatarajia kuongeza nafasi nyingine kwenye baiskeli yangu kwa ajili ya mtoto atakayekuja wiki chache zijazo,”aliongeza. Endapo atajifungua waziri huyo ambaye atachukua miezi mitatu kwa ajili ya mapumziko atakuwa ameongeza idadi ya wanasiasa ambao wamejifungua wakiwa madarakani. Mbunge wa kwanza nchini hapa kujifungua ilikuwa ni mwaka 1970 na mwingine mwaka 1983. Mwaka 2016 Australia ilibadilisha sheria zake kwa kuwaruhusu viongozi wanawake kunyonyesha wakiwa ndani ya bunge. | 2 |
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019 kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza. “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake. | 5 |
JESHI la Polisi Tanzania, Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), limewasilisha mifumo miwili ya teknolojia katika mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na limesema lipo tayari kuipeleka katika nchi zote za jumuiya hiyo zisizo na teknolojia hiyo. Mifumo hiyo iliyobuniwa na wataalamu wa Tehama wa jeshi hilo nchini, ni wa Usimamizi wa Makosa ya Usalama Barabarani na kupata Taarifa ya Upotevu ya Polisi kwa njia ya mtandao bila kulazimika kwenda kituo cha Polisi. Jeshi hilo, Kitengo cha Tehama, Makao Makuu, limeifikisha mifumo hiyo katika mkutano huo unaoendelea jijini Dar es Salaam, unaowahusu mawaziri wa sekta ya Tehama, Habari, Mawasiliano, Uchukuzi (Usafirishaji) na Hali ya Hewa kutoa elimu na kueleza utayari wao kuzisaidia nchi nyingine za SADC. Akizungumza na gazeti hili juzi katika eneo la mkutano huo; Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) walikoweka Banda lao la Jeshi la Polisi, Msimamizi wa Kitengo cha Tehama, makao makuu ya Polisi, Dar es Salaam, Gabriel Mukungu, alisema jeshi hilo lipo tayari kuifikisha mifumo hiyo katika nchi za jumuiya hiyo. “Tuko hapa kuoneshauwezo wa kiteknolojia wa Jeshi la Polisi. Mifumo hii miwili tuliyoileta hapa imebuniwa na vijana wa jeshi wenyewe, hatujanunua kutoka nje. Hatua hii imesaidia pia kupunguza gharama kwa Jeshi la Polisi na kwa wananchi,” alisema Mukungu. Akifafanua kuhusu mifu- mo hiyo, akianza na Mfumo wa Usimamizi wa Makosa ya Usalama Barabarani, Mukungu alisema miaka ya zamani wakosaji wa sheria za usalama barabarani wali- andikiwa faini kwa karatasi (vitabu vya notification) vilivyokuwa vinatengenezwa kwa gharama na kulazimika kusafirishwa mikoa yote kwa magari. Alisema baada ya kuanza kwa mfumo huo Aprili 2017 katika Mkoa wa Pwani na Julai kusambazwa nchi nzima, mabilioni ya Serikali yaliokuwa yakipokea sasa hakuna tena wizi huo kwa kuwa fedha zinapelekwa moja kwa moja serikalini na adhabu imeainisha kosa la dereva na mwenye gari tofuati na awali. “Sasa hivi mtu akikosa, ana nafasi ya kulipa faini ya kosa lake katika kipindi cha siku saba na kwa wanaokiuka utaratibu huo wanageuka kuwa wadaiwa sugu na hukamatwa kwa kamera maalum zinazowekwa barabarani na kuwabana kulipa faini hizo mara mbili ya faini ya awali (penalty),” alisema Mukungu. Kuhusu Taarifa ya Upotevu ya Polisi (Police Loss Report), Mukungu alisema umeanza Julai Mosi mwaka huu na unafanya kazi nchi nzima. Alisema mtu aliyepoteza kitu anaingia moja kwa moja kwenye mtandao wa intaneti kwa tovuti ya https://lormis.tpf. go.tz kusajili taarifa zake za upotevu. “Masharti hapa ni lazima mtu awe na kitambulisho cha taifa. Tumefanya hivi ili kuhimiza kila mwananchi apate kitambulisho hiki kuonesha umuhimu wake. Kwa hiyo kama umepo- telewa na nyaraka kama vyeti, laini ya simu na kadi za benki, hana ulazima wa kwenda Kituo cha Polisi, anaweza kuipata ‘loss re- port’ mtandaoni,” alisema. Akieleza zaidi, Mukungu alisema gharama ya kuipata ni Sh 500 kiasi ambacho watu wengi wanaweza kukipata kwa njia ya simu ya mkononi. Hata hivyo, alisema mtu hatopata taarifa ya upotevu kwa vitu kama kadi ya gari, gari lenyewe na vyombo vya moto, hati za nyumba, mashamba, kampuni, silaha, kifo na mtu kupotea kwa kuepuka hatari ya mwizi wa vitu husika, hawajaziweka mtandaoni kuepuka matumizi mabaya na watu kujihalalishia vitu hivyo. “Kwa aina hii ya upotevu, mtu atalazimika kwenda kituo cha polisi”. Alisema hivi sasa wanaunganisha mifumo hiyo na kampuni za simu ili kurahisisha taarifa kuwafikia kampuni hizo mara moja kama zinavyowafikia Polisi. | 3 |
Na Komba Kakoa-DAR ES SALAAM CHANZO cha kulipuka kwa moto katika bomba la kusambaza gesi eneo la Buguruni kwa Mnyamani, kimetajwa huku ikielezwa kuwa kilisababishwa na wakandarasi wanaoweka bomba la maji la Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco). Taarifa iliyotolewa jana baada ya tukio hilo na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kapuulya Musomba, ilisema pamoja na hali hiyo walifanikiwa kudhibiti moto huo. “Kulitokea moto maeneo ya Buguruni uliosababishwa na bomba la kusambaza gesi viwandani kutobolewa na Excavator, naambiwa ni ya wakandarasi wa uwekaji wa bomba la maji la Dawasco. “Hata hivyo, hali imetulia na kwa muda huu watumia gesi viwandani wanaanza kurudishiwa na sehemu iliyotobolewa itaangaliwa vizuri ili kukarabatiwa,” alisema Musomba katika taarifa yake na kutoa pole kwa waathirika wa tukio hilo. USHUHUDA Akizungumza na MTANZANIA iliyofika katika eneo hilo jana na kuzungumza na mashuhuda wa tukio hilo, Athuman Ramadhan, alisema kuwa waliwaona mafundi hao wakichimba mtaro na kuwaambia wanatakiwa kuchukua tahadhari kwani eneo hilo limepita bomba la gesi. Alisema hata walipowaambia, lakini bado mafundi hao waliendelea na kazi hiyo ndipo walipojikuta wakikwama baada ya kutoboa bomba hilo la gesi na moto kuanza kulipuka. WAATHIRIKA WAIBIWA Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Faru, Simba Said, alisema tatizo hilo limechangiwa na dereva wa tingatinga kukosa mawasiliano mazuri na wananchi ambao walimpa tahadhari kabla. “Licha ya kutokuwa na mawasiliano mazuri, lakini pia hao mafundi wanaonekana ni jeuri, kwani eneo hilo kuna alama zinazotahadharisha, lakini walijifanya wataalamu hatimaye wakatoboa bomba la gesi na kusababisha athari kubwa,” alisema Said. Aidha alisema kuwa amesikitishwa na kitendo cha baadhi ya vijana kuingia kwenye baadhi ya nyumba katika eneo hilo na kuanza kuiba mali za waaathirika wa moto huo. “Inasikitisha kuona baadhi ya wenzetu wakifurahia mateso ya wenzao na kuamua kuwaibia, jambo hili halivumiliki, tutawatafuta na kuwakamata, naomba Jeshi la Polisi watusaidie pindi tutakapohitaji msaada wao,” alisema mwenyekiti huyo. WAATHIRIKA Mmoja wa waathirika, Hassan Simba, ambaye nyumba yake imeteketea kwa moto, alisema hana la kufanya kwa sasa kwani hakuna kitu chochote alichookoa ndani ya nyumba yake. “Sijui nifanyeje kwani baada ya kupokea taarifa na kufika nyumbani, sikuweza kuokoa kitu hata kimoja, nilikuta wapangaji na familia yangu wakilia wasijue kitu cha kufanya,” alisema Simba. VIONGOZI WANENA Diwani wa Vingunguti, Omary Kumbilamoto (CUF), alisema kuwa kilichotokea kwenye eneo hilo ni uzembe wa mamlaka kutowasiliana kwani wahusika walitakiwa kukaa kabla ya kuanza kwa ujenzi huo. Kumbilamoto ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, alisema kuwa amesikitishwa na tukio hilo huku akitaka hatua zichukuliwe kwa waliolisababisha. Kutokana na tukio hilo, Mbunge wa Segerea, Bonnah Kaluwa (CCM), alifika katika eneo hilo na kutoa pole kwa waathirika na alisema kwa sasa wataalamu wanaendelea kufanya tathimini. Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, alifika katika eneo hilo na kusema kuwa familia moja yenye watu 13, itakuwa chini ya uangalizi wa Manispaa ya Ilala wakisubiri tathmini inayofanywa na wataalamu. MAJERUHI WATATU Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya Buguruni, Dk. Isack Makundi, alisema alipokea mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo ambaye ni mtoto. “Juzi tulipokea majeruhi mmoja ambaye ni mtoto, akiwa ameungua zaidi kichwani. Hata hivyo baada ya huduma tulimhamishia Hospitali ya Amana na leo (jana) asubuhi tumepokea majeruhi wengine wawili, mwanamke na mwanaume wakiwa wameungua mikononi na mgongoni ila kwa sasa wanaendelea vizuri,” alisema Dk. Makundi. MTOTO APOTEA Katika ajali hiyo, ilielezwa kuwa mtoto Shukuru Yahaya (14), amepotea na hajulikani alipo. Akieleza tukio hilo, kaka wa mtoto huyo, Selemani Yahaya, alisema mdogo wake hawakumwona tangu moto ulipolipuka katika eneo hilo. Alisema baada ya tukio hilo mdogo wake alikurupuka mithili ya mtu aliyerukwa na akili na kuanza kukimbia ovyo na hadi jana jioni bado alikuwa hajapatikana. | 3 |
Na CHRISTINA GAULUHANGA-DAR ES SALAAM JAMII imetakiwa kuwasaidia wenye matatizo mbalimbali kwa kuwawezesha vifaa vya kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 ambao unasababishwa na virusi vya corona. Diwani wa Kata ya Ukonga, Jumaa Mwipopo, akizungumza wakati akipokea msaada wa barakoa kwa watu wenye mahitaji maalumu, alisema jamii inatambua adha ya ugonjwa huo, hivyo ni vema kuwalinda watu wenye mahitaji maalumu. Alisema kata hiyo ina wazee wengi wasiojiweza na wajane, hivyo wanahitaji misaada ya hali na mali ili waweze kujikimu kimaisha na kuwakinga wasipate maambukizo ya ugonjwa huo. “Natumia fursa hii kumshukuru Neema Edward ambaye ni mlemavu lakini ameguswa na wengine wenye shida na kuamua kutoa alichonacho kama sadaka yake kwa Mungu,” alisema Mwipopo. Pia aliomba Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kufikiria kuongeza muda wa riba kwa vikundi vya wajasiriamali vya kina mama walemavu kwakuwa kipindi hiki cha Covid-19 wengi hawajafanya biashara. Akikabidhi msaada huo, Neema alisema ameguswa na hali ya kimaisha waliyonayo wengine, hivyo kupitia ofisi yake ya Mkwelele Wellness Foundation, ameamua kutengeneza barakoa na kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu. Alisema anatambua gharama za kununua barakoa, hivyo ana imani kidogo alichokitoa kitasaidia kuokoa maisha ya watu endapo hawataambukizwa na maradhi mbalimbali. “Natambua adha ambazo wanazipata watu wenye ulemavu pamoja na wazee, kwakuwa barakoa zimekuwa zikiuzwa kwa gharama kubwa, hivyo kwa nafasi yangu nimeona kidogo nilichonacho kitasaidia kupunguza matatizo waliyonayo,” alisema Neema. Aliwataka wajasiriamali wengine na taasisi mbalimbali kuendelea kuliwezesha kundi hilo ambalo wengi wao hawana msaada kutoka kwenye familia zao. | 3 |
Taifa Stars imefanikiwa kuvuka hatua nyingine baada ya kuifunga Malawi kwa juma ya mabao 2-1, wakifunga mabao 2-0 nyumbani na kufungwa bao 1-0 ugenini. Akizungumza juzi baada ya mchezo dhidi ya Malawi uliochezwa kwenye uwanja wa Kamuzu Banda jijini Blantyre Malawi, Morocco alisema wanashukuru kwa kufanikiwa kuitoa Malawi, kwani wanarudi kujipanga tena kwa ajili ya kuwamaliza Algeria.Alisema licha ya kuwa Algeria ni timu bora Afrika, ikiwa watajipanga wanaweza kufanya vizuri na kuwapindua. “Tunashukuru kuvuka hatua moja bado tuna kazi ngumu na kubwa mbele yetu kuhakikisha tunaendeleza ushindi katika mchezo ujao na kutengeneza historia mpya katika soka letu,” alisema.Hatua hiyo imeifanya Stars kutengeneza historia mpya ya kuifunga Malawi, kwani kwa kipindi cha karibu mwaka mzima walichokuwa wakikutana katika michezo ya kirafiki walikuwa wakitoka sare, ambayo kama siyo ya kufungana basi ya kutokufungana.Ushindi huo ni mwanzo mzuri wa Kocha Mkuu Charles Mkwasa na benchi lake la ufundi ikiwa ni siku chache tangu kukabidhiwa mkataba wa kudumu wa kuinoa timu ya Taifa. Kulingana na viwango vya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Tanzania inashika nafasi ya 136 wakati timu waliyoitoa inashika nafasi ya 101 na timu wanayotarajia kukutana nayo ya Algeria ikishika nafasi ya 19 kwa ubora duniani huku ikiwa ya kwanza Afrika.Taifa Stars ilitarajiwa kuwasili jana ikitokea Malawi huku wachezaji walioko katika kikosi hicho wakisubiriwa na timu zao kujiandaa na michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoendelea mwishoni mwa wiki ijayo. | 4 |
*Mkwasa atamba kuifunga Malawi, apewa mkataba mnono
*Lowassa aitakia ushindi, adai utaongeza hamasa Tanzania NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Mkwasa, amewahakikishia Watanzania mabadiliko
makubwa wakati timu hiyo itakapomenyana na Malawi leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Stars itakuwa mwenyeji wa Malawi katika mchezo wa hatua ya awali ya mtoano wa mashindano ya kuwania kufuzu
Fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi. Stars chini ya Mkwasa haijaambulia ushindi kwenye mechi tatu zilizopita alizoanza kuinoa timu hiyo, akianza kwa
kutoa sare dhidi ya Uganda (1-1), akafungwa na Libya (2-1) kwenye mechi ya kirafiki kabla ya kutoa suluhu na Nigeria. Mkwasa ataingia kwenye mchezo huo akiwa na morali kubwa baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kumpa
mkataba wa kudumu wa mwaka mmoja na nusu kuinoa timu hiyo unaoanzia Oktoba Mosi, mwaka huu hadi Machi 31, 2017. Mkataba huo unamwezesha Mkwasa kupata huduma zote na marupurupu aliyokuwa akipewa mtangulizi wake Mholanzi, Mart Nooij, aliyetimuliwa kutokana na matokeo mabaya, ikiwemo nyumba, gari na mshahara wa Sh
milioni 25 kwa mwezi, sawa na Dola za Kimarekani 12,500. Mkwasa, aliyefurahishwa na makubaliano yaliyofikiwa na TFF, ataweza kuvuna kiasi cha Sh mil 450 kwa kipindi cha miezi 18 ya mkataba huo, huku akiahidi kufanya jitihada kuongeza kiwango cha Stars. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkwasa alisema mchezo huo utakuwa mgumu, lakini wamejiandaa kupambana ili
kuibuka na ushindi nyumbani, huku akisisitiza dakika 90 zinatosha kuleta mabadiliko ya soka nchini. “Dakika 90 zitaweza kuleta mabadiliko na kutupatia ushindi ambao ni muhimu kwetu, kwani ninawafahamu vizuri Malawi kwa kuwa soka lao halina tofauti na kwetu,” alisema. Stars itaingia dimbani ikichagizwa na moto wa washambuliaji wake wa kulipwa, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, waliofanya vizuri kwa siku za hivi karibuni wakiwa na TP Mazembe, iliyotinga fainali ya Ligi
ya MMabingwa Afrika, pamoja na Mrisho Ngassa aliyeanza kung’ara akiwa Free States Stars ya Afrika Kusini. | 4 |
SERIKALI imeanza kugawa ekari 972,500 za ardhi kwa wafugaji wanaotangatanga kutafuta malisho ya mifugo ili kumaliza kabisa migogoro baina yao na wakulima iliyodumu kwa miaka mingi na kusababisha uvunjifu wa amani.Pia wafugaji wengi walipata hasara kwa mifugo yao kutaifishwa, kutozwa faini na hata mingine mingi kufa kutokana na kukamatwa kisha kushikiliwa kwa muda mrefu bila huduma muhimu ikiwemo maji, malisho na matibabu kwenye hifadhi mbalimbali za taifa nchini.Akizindua ugawaji wa ardhi hizo kwa wafugaji nchini katika Ranchi ya Kalambo wilayani Nkasi mkoani Rukwa, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina alisema uamuzi huo wa serikali umekuja kutokana na wafugaji wengi nchini kuhangaika kila mahali kutafuta malisho na kusababisha migogoro mingi baina yao na wakulima. Hivyo kwa upande wa Ranchi ya Kalambo, wafugaji wamegawiwa ekari 25,000 zenye uwezo wa kuhifadhi mifugo 6,000, na hadi sasa jumla ya ng’ombe 3,000 wameshaingia kwenye ranchi hiyo wakati serikali na wafugaji wenyewe wakiendelea kutafuta suluhisho la kudumu la kupata malisho.Waziri Mpina amewataka wafugaji wanaohangaika kutafuta malisho kutumia fursa hiyo ya serikali ya uwepo wa maeneo ya kulishia mifugo ili wawe karibu na huduma za tiba na chanjo pindi mifugo yao inapopata maradhi.Aidha, aliipongeza kamati maalumu aliyoiunda ya kutatua migogoro ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi kwa kufanikisha upimaji na ugawaji wa ardhi hiyo kwa wafugaji pamoja na kutatua migogoro yote iliyokuwepo baina ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi katika mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.Pia alimwagiza Katibu Mkuu Mifugo kuhakikisha ukarabati wa kituo cha uchunguzi wa magonjwa ya wanyama cha Kanda ya Kusini Magharibi kinakamilika ifikapo Februari mwakani ili mikoa ya Katavi na Rukwa kutokuwa na kituo hicho licha ya kuwepo mifugo mingi.Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk Halfan Haule alisema kutokuwepo kwa maeneo ya malisho na maji ya kutosha kwa ajili ya mifugo kumekuwepo na migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi na kumshukuru waziri kwa uamuzi wa kugawa vitalu kwa wafugaji.Pia alisema Mkoa wa Rukwa umekuwa ukikabiliwa na magonjwa ya mifugo ikiwemo homa ya nguruwe (ASF), Homa ya Mapafu ya Ng’ombe (CBPP), Homa ya mapafu ya mbuzi (CCPP), Ugonjwa wa miguu na midomo (FMD), Ugonjwa wa mapele ngozi (LSD), Ugonjwa wa kichaa cha mbwa na ugonjwa wa mdondo (ND).Katibu wa Umoja wa Wafugaji Ranchi ya Kalambo, Benuel Benzeth aliishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli, kwa uamuzi wake wa kugawa maeneo hayo ya serikali kwa wafugaji katika kipindi ambacho wanaendelea kutafuta suluhisho la kudumu la changamoto ya malisho.Benzeth alisema mifugo yao mingi imekufa na mingine kudhoofika kutokana na kukamatwa na kushikiliwa kwenye hifadhi bila matunzo na wakati wote serikali haijawahi kuchukua hatua za kuwasaidia wafugaji na kumshukuru waziri kwa uamuzi huo ambao umewezesha mifugo mingi kupona na kuendelea na uzalishaji.Awali akizungumza baada ya kutembelea Kiwanda cha Nyama cha SAAFI mjini Sumbawanga mkoani Rukwa, Waziri Mpina alisema serikali inafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kiwanda hicho kinaanza kufanya kazi haraka ili kusaidia upatikanaji wa mifugo takribani milioni sita iliyoko Rukwa, Katavi, Songwe na Mbeya. | 3 |
SERIKALI za Tanzania na Malawi zimesema zitahakikisha zinasimamia kwa karibu mradi wa kamisheni ya Mto Songwe kwa lengo la kukamilisha mawazo ya waasisi wa mataifa hayo, Mwalimu Julius Nyerere na Kamuzu Banda ya kuutumia mto huo kuwanufaisha wananchi wao.Naibu Waziri wa Maji nchini, Jumaa Aweso na Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji na Maendeleo ya Maji wa Malawi, Joseph Mwanamvekha, walieleza nia hiyo kwenye hafla ya uzinduzi wa Kamisheni ya Mto Songwe iliyofanyika mjini Kyela mkoani Mbeya, na kuhudhuriwa na maofisa wa ngazi mbalimbali wa serikali za Tanzania na Malawi.Aweso aliyemwakilisha Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa alisema wizara haiko tayari kuona mpango wa kamisheni hiyo unakufa na kwa kuwa wamefikia hatua ya kuzindua kuanza kwa mradi, ni wakati wa pande zote mbili kufunga mkanda ili kutimiza malengo.“Kama wizara niwahakikishie kuwa hatutorudi nyuma tena…tutahakikisha mradi unafanyika na hatimaye wananchi wetu wa nchi hizi mbili wanufaike kama waasisi wa mataifa yetu walivyotaka,” alisema Aweso.“Miongoni mwa faida zitakazopatikana kwa kupitia mradi huu ni pamoja na wananchi kuwa na fursa ya kuendesha shughuli za kilimo cha umwagiliaji, uvuvi, kuzalisha umeme kupitia mabawa makubwa yatakayojengwa na pia kupata maji kwa matumizi ya majumbani.”Aliwataka wananchi waishio katika wilaya zitakazonufaika na mradi huo kuanza kujiandaa kwa kubuni shughuli mbalimbali zitakazowawezesha kuwa sehemu ya wanufaika wa mradi husika badala ya kubweteka.Mwanamvekha alisema ni jambo linalotia faraja kwa hatua iliyofikiwa kwani mradi huo pia utakuwa chachu ya mahusiano mema baina ya Tanzania na Malawi kwa kuwa utafungua fursa za pamoja na kunufaisha wananchi.“Safari ya mpango huu ilikuwa ndefu, lakini tunashukuru kwa hatua hii tuliyofikia. Nina hakika watu wetu walisubiri kwa muda mrefu kunufaika na mradi huu na sasa ndoto zao za muda mrefu zinakwenda kutimia,” alisema Mwanamvekha.Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo alisema serikali za pande zote mbili zimejipanga kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika kuhakikisha mradi haukwami, bali ujengwe kwa wakati uliopangwa.Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alisema wamejipanga kupitia wataalamu wao kuhakikisha wanashiriki ipasavyo kwenye kamisheni, na kusisitiza ushirikiano baina ya Watanzania na Wamalawi ni muhimu kuendelezwa.Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Claudia Kita alisema hali ya amani na utulivu iliyopo katika mikoa ya Mbeya na Songwe nchini na Kalonga nchini Malawi ni chachu ya mradi husika hivyo atahakikisha kuwa kutakuwa na manufaa ya muda mrefu. | 3 |
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe, amewaomba Watanzania kuichangia Timu ya Taifa (Taifa Stars) ambayo ipo Misri kwa ajili ya Michuano ya Mataifa Afrika (AFCON) mwaka 2019 Mwakyembe amesema hayo leo Jumatatu, Juni 17, 2019 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu maandalizi ya Stars ykwa ajili ya fainali za AFCON. “Siku ya Alhamisi asubuhi tutakuwa na zoezi kubwa ambalo litaluwa LIVE kwenye mitandao na television mbalimbali na kwenye radio ambapo tutafanya uchangiaji wa Taifa Stars. Nawahakikishia kila shilingi itakayopatikana itakwenda kwa vijana wetu, wasishindwe kwa kuvunjika moyo,” amesema. Amesisitiza kwamba fedha zitakazochangwa si kwa ajili ya kuipeleka timu Misri na kuirudisha, “hatuhitaji kuwaweka kwenye hoteli nzuri (hayo yote yameshafanyika) tunahitaji kufanya kitu ili timu yetu ifanye vizuri. “Leo hii Tanzania inajivunia kwamba ukitaja ma-striker wakubwa duniani huwezi ukamkosa Samatta, Mungu atupe nini? Ndiyo kipindi chetu, dunia sasa hivi inatambua Tanzania ipo mpaka hapa tulipofikia,” amesema Dkt. Mwakyembe.
| 4 |
KIEV, UKRAINE MCHEZAJI bora duniani, Cristiano Ronaldo, juzi aliandika historia mpya ya
kufikisha jumla ya mabao 700 aliyoyafunga katika maisha yake ya soka la
kulipwa. Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa Ureno, alifunga bao moja kwenye mchezo wa
kuwania kufuzu michuano ya Euro 2020, lakini Ureno ilikubali kichapo cha mabao 2-1
dhidi ya Ukraine. Ronaldo ambaye anakipiga katika klabu ya Juventus, alisema kitendo cha
kuweka rekodi mbalimbali kinakuja chenyewe. Bao hilo la 700 alilifunga kwa
mkwaju wa penalti kipindi cha pili cha mchezo huo. Hata hivyo Ureno ilikubali kichapo hicho ambacho ni chakwanza kukipata tangu
kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi mwakani jana. “Kufikisha idadi hii ya mabao sio kama kila mchezaji anaweza kufanya, lakini
nitumie nafasi hii kuwashukuru wachezaji wenzangu, makocha kwa kunifanya niwe mchezaji
kama nilivyo sasa. Mbali na kufurahia rekodi hii, lakini nimechukizwa kwa
kitendo cha kushindwa kupata ushindi dhidi ya wapinzani,” alisema mchezaji
huyo. Hata hivyo alipoulizwa juu ya mafanikio yake mwenyewe, Ronaldo alisema, “Kwani
nina rekodi ngapi hadi sasa? Sijui, lakini natakiwa kufurahia hali hii na
kuwashukuru wale wote ambao wamenifanya niwe hapa. | 2 |
MKUU wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme amefungua rasmi msimu mpya wa korosho kwa kuwataka wanunuzi wa zao hilo kujiepusha na hujuma kwa wakulima. 'Aidha, amepiga marufuku ununuzi wa zao hilo kwa mfumo wa kangomba aliouita haramu. Mndeme alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha wadau wa zao hilo kilichofanyika mjini Tunduru.Aliitaka Bodi ya Korosho Tanzania kuendelea kuhamasisha maendeleo ya zao hilo kwani azma ya serikali ni kuona kuna maeneo mapya na mengi zaidi ya uzalishaji na ya asili yanazingatia kanuni za kilimo bora na cha kisasa ili kuleta tija katika zao hilo.Alisema ni wakati muafaka sasa kwa wadau mmoja mmoja, vikundi na taasisi kuchangamkia fursa hiyo ya kiuchumi kwa kujenga viwanda vya kubangua korosho katika mkoa wa Ruvuma kwani hatua hiyo itasaidia kuongeza thamani ya zao hilo na kuwaongezea kipato cha wakulima.Msimu wa masoko na mauzo ya korosho wa mwaka 2018/2019 ulishafunguliwa tangu Oktoba mosi mwaka huu, hata hivyo korosho zilizopelekwa mnadani zilishindwa kuuzwa kutokana na bei iliyopatikana katika minada hiyo kutokidhi matarajio ya bei kwa wakulima.Mndeme alisema uamuzi wa serikali kununua korosho katika msimu 2018/2019 ulikuwa ni hatua ya dharura iliyochukuliwa ili kulinda maslahi ya mkulima na wananufaika kwa kupata bei nzuri kulingana na mwenendo wa soko.Aliwataka watunza maghala kuwa waadilifu, waaminifu na waepuke udanganyifu wa upimaji wa korosho za wakulima na inapotokea tofauti kubwa ya uzito, kazi ya kupima mzigo huo isimame mpaka serikali au mamlaka husika itakaposhirikishwa kwa ajili ya utatuzi.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro alisema atasimamia utaratibu wa ununuzi wa korosho za wakulima na kuwataka watu kujiepusha na biashara ya kangomba inayochangia dhuluma na wizi dhidi ya wakulima.Meneja wa Bodi ya Korosho, tawi la Tunduru, Shauri Mokiwa alisema msimu wa masoko na mauzo ya korosho ghafi nchini ulifunguliwa rasmi kitaifa Oktoba mosi 2018 na Oktoba 3 mkoani Ruvuma. Alisema mfumo wa mauzo uliotumika ni wa stakabadhi ghalani ambao katika minada iliyoendeshwa awali mwanzo wa msimu katika mkoa wa Ruvuma wakulima hawakuweza kuuza korosho, kutokana na bei kuwa ndogo ambayo ilikuwa kinyume cha matarajio yao ikilinganisha na bei zilizopatikana katika msimu wa 2017/2018.Katika msimu wa mauzo ya korosho ya mwaka 2018/2019 kiasi cha korosho kilichokusanywa kupitia Chama Kikuu cha Ushirika (TAMCU) ni tani 18,586.448 za mkoa wa Ruvuma na tani 64.032 za mkoa jirani wa Njombe na kuuzwa, ikiwa ni pungufu ya asilimia 28.7 ya makisio ya makusanyo ya msimu 2018/2019 ya tani 26,000.Alisema, kiasi hicho za uzalishaji kimeshuka kwa asilimia 11.12 ikilinganisha na uzalishaji wa tani 20,912.569 kwa msimu 2017/2018 ambapo hali hiyo ilitokana na sababu mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya hali ya hewa, matumizi hafifu ya viuatilifu, ufinyu wa elimu ya matumizi sahihi na salama ya viuatilifu. | 3 |
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam JESHI la Polisi Mkoa wa Ilala limefungua madawati tisa katika vituo vikubwa vya polisi na vya kati kwa ajili ya kuwahudumia wanawake na watoto wanaonyanyaswa kijinsia. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni, wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa jinsia dhidi ya wanawake na watoto. Alisema wameandaa maandamano ya amani yatakayoanzia Tazara kuelekea Vingunguti katika Viwanja vya Shule ya Msingi Vingunguti na mgeni rasmi atakuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema. Pia alisema katika kupambana na ukatili wa jinsia, wameanzisha madawati katika ofisi ya RPC Ilala, Wilaya ya Kati, Kariakoo, Stakishari, Buguruni, Pangani, Tabata, Salenda Bridge na Vingunguti. Alisema makosa mengi yamekuwa yakiripotiwa katika maeneo yote na alitoa mfano kuwa mwaka jana kesi 633 za unyanyasaji wa jinsia na ukatili ziliripotiwa na kuanzia Januari hadi Septemba, mwaka huu kesi 1,094 zimeripotiwa. Alisema kesi hizo zimeripotiwa baada ya kupata taarifa za siri kutoka kwa raia wema na kwa upande wa migogoro ya ndoa wametoa rufaa kwenda manispaa kitengo cha ustawi wa jamii. Kwa mwaka jana, alisema jumla ya kesi 52 zilipewa rufaa na mwaka huu kesi 70 zilipewa rufaa. “Makosa ya jinai yaliyojitokeza kila wakati ni kulawiti, kubaka, vipigo, shambulio la aibu, shambulio la kudhuru mwili, lugha ya matusi na shambulio la kawaida, kesi hizo ziko katika hatua mbalimbali. “Zingine ziko kwa mwanasheria, zingine mahakamani na upelelezi wa kesi nyingine hazina muendelezo baada ya jamii kuripoti na kutotokea kuendelea na kesi hizo,” alisema Hamduni. | 3 |
['Wanariadha mara nyingi wana kitu kinachowasukuma kufanikiwa, na kwa mbio za marathon za wanawake hata kuweka rekodi ni matokeo ya msukumo alioupata Brigid Kosgei alipokuwa akipitia kipindi kigumu utotoni.', "''Nikifikiri kuhusu nilikoanzia na changamoto tulizopitia tulipokuwa tunakua, ninajiambia siwezi kurudi kwenye maisha yale yale na hicho kilinisukuma kufanya vizuri , ''mwanariadha huyu aliambia BBC.", 'Miaka minne tangu aliposhiriki kwa mara ya kwanza mbio za marathon, ambazo alishinda, Kosgei kwa sasa ni mwanamke mwenye mbio zaidi katika historia kwa umbali wa kilometa 42.2', 'Juma lililopita katika mji wa Chicago nchini Marekani, alivunja rekodi iliyowekwa na muingereza Paula Radicliffe aliyoiweka miaka 16 iliyopita.', 'Alikuwa mmoja kati ya watoto saba waliolelewa na mama pekee katika kaunti ya Elgeyo -Marakwet, mji katika bonde la ufa ambao umewatoa wakimbiaji maarufu wa nchini Kenya.', 'Na kama ilivyo kwa wakimbiaji wengine wa Kenya kabla yake, Kosgei aligundua kuwa anaweza kukimbia akiwa shule ya msingi, ambapo alikuwa akikimbia kwenda darasani nyakati za asubuhi.', "''Shule yangu ilikuwa umbali wa kilomita 10 kutoka nyumbani na wakati mwingine kuepuka kuchelewa nilikua nakimbia, nikiwa njiani nilikutana na wakimbiaji wakiwa mazoezini na kujisemea mwenyewe: 'ninaweza kuwa kama wao' alisema.", 'Alianza kushindana kwa umbali wa kati akiwa shuleni na ingawa hakuchaguliwa kuwakilisha nchi yake, kipaji chake hakikuwa na shaka.', 'Baada ya kuongezwa kwa karo ya shule ilikuwa changamoto kwa mama yake, Kosgei aliamua kukatisha masomo yake mwezi Januari mwaka 2012 katika mwaka wake wa mwisho.', "''Nilipofika kidato cha tatu, malimbikizi ya madeni yalikua zaidi ya pauni 1,200. Mama yangu alijaribu kunishawishi niendelee na shule naye atakopa fedha kulipa deni nilimwambia: ''kwa muda gani utaendelea kukopa?''", 'Ghana, Senegal na Ivory Coast zaondolewa CHAN', 'Eliud Kipchoge atuzwa shujaa wa taifa', 'Lakini sasa akiwa na miaka 17, aliutilia maanani mchezo wa kukimbia- kazi ambayo iliiwezesha familia kuwalipia karo ndugu zake wadogo.', 'Alianza kufanya mazoezi na rafiki yake wa kiume Mathew Kosgei, ambaye kwa sasa ni mumewe. Mwaka mmoja baadae alikua mapumzikoni baada ya kujifungua watoto mapacha.', 'Lakini uzazi haukumfanya akatishe nia yake. Mwaka 2015 alianza alipoishia, wakati huu aliingia kwenye kambi ya mafunzo si mbali na makazi yake, kambi iliyokuwa chini ya mwalimu wake.', 'Kambi hizo nchini Kenya zinatoa mazingira ambapo wakimbiaji wanapata nafasi ya kujikita zaidi na mafunzo bila kuingiliwa.', '', 'Brigid Kosgei:women’s marathon record holder ', 'Vivian Cheruiyot: 2011 double world champion; Olympic gold and silver in 2016', 'Wilson Kipsang:former marathon world record holder', 'Ezekiel Kemboi:2004 and 2012 3,000m steeplechase Olympic champion', "Saif Saeed Shaheen:Men's 3,000m steeplechase record holder; 2003/2005 champion", 'Lornah Kiplagat:2007 world champion in cross country', 'Msimu wake sasa umepita lakini amerekodiwa kuwa mkiambiaji wa kwanza mwanamke wa marathon kwa mwaka 2019. Mwaka ujao amedhamiria kushiriki michuano mikubwa zaidi ya Olimpiki.', 'Kwa sasa anaelekea kijijini kumtembelea mama yake, ambaye amemnunulia kiwanja na nyumba kutokana na faida aliyopata aliposhinda michuano kadhaa awali, pia atatumia muda huo akiwa na mumewe na watoto.'] | 4 |
Msanii wa Filamu nchini Elizabeth Michael maarufu kama (Lulu) ameamua kubadilisha mwonekano wake wa nyweli huku akiyataja maazi hayo kuwa ni mazito kwake. Lulu ambaye inasemekana hivi karibuni alijifungua mtoto ambaye amemzaa na mpenzi wake wa sasa Majizo, ameposti picha akiwa amenyoa nyweli na kupaka brichi ya rangi ya dhahabu. Ni Mimi Huyu Last Born Wa Defao 🤗💃 . . . #donttrythisathome🤣 #maamuzikamahayayanahitajikujizimadata🤣 A post shared by Elizabeth Michael (@elizabethmichaelofficial) on Jan 9, 2020 at 9:22am PST Mwenyewe ameandika kuwa ni maamzi ambayo yanahitaji mtu azime data kwanza huku akiwasisitiza wengine kutonajaribu. Hata hivyo si mara ya kwanza kwa Lulu kuwa na nyweli fupi ila ni mara ya kwanza kuonekana zikiwa na rangi hiyo kwa kimo kile. Katika posti yake ya kwanza katika muonekano huo aliyoiweka katika mtandao wa Instagramu watu zaidi ya 50,000 wameifurahi na zaidi ya 1000 wamekommenti. Nawe unaweza kutuandikia Kommenti yako chini hapo juu ya maamzi hayo ya staa wa Filamu. | 1 |
NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye ulemavu, Antony Mavunde ameamua kumfanya sehemu ya familia yake, mtoto Christopher Alex (10) aliyekatwa miguu baada ya kuugua ugonjwa uliosababisha miguu iharibike.Akizungumza juzi jijini hapa kwenye Hospitali ya Benjamin Mkapa, alisema aliguswa baada ya kusikia taarifa za mtoto huyo, hivyo atamfanya mtoto huyo kuwa sehemu ya familia yake kugharamia mahitaji yake ya msingi na kumnunulia miguu bandia."Tunapaswa kuwa sehemu ya utatuzi wa changamoto zinazowakabili wenye mahitaji na kuacha kuchangia mambo yasiyokuwa na uhitaji kwenye jamii, Nitakuwa nikiwasiliana na mzazi wake kuhakikisha anapata huduma zote muhimu ikiwemo kuendelea na masomo. Nataka mtoto huyo awe mfano katika kutimiza ndoto zake," amesema.Mavunde ambaye pia ni Mbunge wa Dodoma Mjini (CCM) alisema madaktari kutoka Dar es Salaam walikuwa wanatarajia kuwasili mjini hapa kwa ajili ya kuchukua vipimo vya kutengeneza miguu ya bandia.Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dk. Alphonce Chandika amesema baada ya kufanyiwa uchunguzi mtoto huyo alibainika miguu yake imeharibika kuanzia chini ya magoti."Hivyo hakukuwa na jinsi zaidi ya kuikata, tulifanya hivyo kwa kukata mguu moja baada ya mwingine, baada ya matibabu ya wastani wa mwezi mmoja na nusu sasa anaruhusiwa kurudi nyumbani,”amesema.Amesema kutokana na hali ya mtoto huyo, hospitali ya Benjamin Mkapa imempatia kiti cha magurudumu ambacho atakitumia baada ya kuruhusiwa.Akizungumzia tatizo la mtoto huyo, mjomba wa mtoto huyo, Ludovick Julius amesema mtoto huyo alianza kwa kusumbuliwa na tatizo la upungufu wa damu mwilini. "Tulimpeleka Hospitali ya Mvumi lakini madaktari wakasema kwa tatizo lake anapaswa kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma."Tulipofika hospitali ya mkoa, Juni 11 mwaka huu ilibanika miguu yake imeharibika kwani alivimba mwili mzima na baadaye uvimbe huo ulikwisha lakini ulisalia miguuni pekee"amesema.Julius ambaye pia ni mlemavu wa ngozi, anaeleza baada ya hali hiyo madaktari walishauri mtoto huyo akatwe miguu lakini familia iliamua kwenda Hospitali ya Benjamin Mkapa ili apatiwe matibabu.Hata hivyo, alisema uchunguzi ulifanywa na madaktari wa hospitali hiyo walibaini miguu haiwezi kutengemaa hivyo, inapaswa kukatwa. | 3 |
TAASISI zinazohusika na utozaji kodi katika sekta ya madini zimeonywa na kutakiwa kuacha mara moja kutoza kodi zote zilizofutwa na serikali katika sekta hiyo. Waziri wa Madini, Dotto Biteko alitoa onyo hilo jana bungeni na kusema ni marufuku kutoza kodi ambazo zimefutwa na Bunge katika sekta hiyo.“Natoa wito kwa watozaji kodi kuacha kutoza kodi za sekta za madini ambazo zimefutwa kisheria humu bungeni ...kodi zote zilizofutwa na serikali, hakuna mtu mwingine kuzitoza, kinyume na hapo anakiuka taratibu za serikali,” alisema Biteko.Biteko alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mombo, David Silinde (Chadema) aliyesema kodi zinazotozwa kwa wachimbaji wadogo ni nyingi. Awali, Naibu Waziri wa Nishati Stanslaus Nyongo alitoa wito kwa mchimbaji mdogo yoyote mwenye malalamiko ya msingi kutoa taarifa kupitia Ofisi za Madini zilizoko mikoani ili yaweze kushughulikiwa kwa mujibu wa Sheria. Nyongo alikuwa akijibu swali la msingi la mbunge wa viti maalum, Rhoda Kunchela aliyehoji iwapo serikali iko tayari kutatua kero kwa wachimbaji wadogo na vibarua ambao wananyanyasika katika migodi mbalimbali hapa nchini.Alisema serikali imedhamiria kuondoa kero kwa wachimbaji wadogo hasa za maeneo ya kuchimba ili kuwawezesha kujiajiri katika sekta ya madini. Aidha, aliagiza Tume ya Madini kuhakikisha wamiliki wote wa leseni za utafiti ambazo hazifanyiwi kazi zifutwe ili maeneo hayo wamilikishwe wachimbaji wadogo wenye lengo la kuviendeleza ili kuongeza mchango wa sekta ya madini katika pato la taifa na kujenga uchumi wa viwanda. Nyongo alisema aina yoyote ya unyanyasaji wa aina yoyote haikubaliki na mmiliki yoyote anayefanya hivyo atakuwa kavunja sheria ya madini na sheria za kazi mahali pa kazi. | 3 |
KOCHA Msaidizi wa Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Simba, Masoud Djuma amesema anatamani kukutana na Gor Mahia kwenye fainali ya michuano ya Kombe la Kagame inayotarajia kuanza kutimua vumbi Juni 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.Simba ilipoteza kwa magoli 2-0 dhidi ya Gor Mahia, katika mchezo wa fainali wa michuano ya SportPesa Super Cup, iliyoshirikisha timu nane iliyofanyika hivi karibuni mjini Nakuru, Kenya. Akizungumza na gazeti hili jana, Djuma alisema kitu cha msingi anachokifanya kwa sasa ni kurekebisha mapungufu aliyoyaona kupitia kwenye michuano hiyo ili wacheze fainali za Kagame kama walivyokusudia.“Lengo langu kubwa ni kucheza fainali na Gor Mahia ili kulipa kisasi kwa sababu walitufunga kwenye fainali ya SportPesa kule kwao Kenya, tulikuwa na mapungufu lakini tupo kwenye maandalizi kabambe ya kuhakikisha tunabakiza taji Tanzania,” alisema Djuma. Kocha huyo alisema amewaita wachezaji wake wote kuingia kambini ili kuanza maandalizi ya michuano hiyo ambayo pia alisema ataitumia kama kipimo cha kuwajaribu wachezaji wake waliosajiliwa kwa msimu ujao.Alisema anatambua kuwa msimu ujao wa ligi watakuwa na changamoto kubwa ya kutetea taji lao kutokana na mafanikio waliyopata msimu uliopita hivyo wanalazimika kujenga kikosi imara kitakachopambana kupata matokeo bila kuhofia timu yoyote ndani na nje ya nchi. Simba ndiyo bingwa wa kihistoria wa michuano hiyo ya Kombe la Kagame, ikilitwaa mara sita na kuzipiku timu nyingine kubwa zikiwemo watani zao wa jadi Yanga ambao wamelibeba mara tano. Yanga haitashiriki michuano ya mwaka huu baada ya kujitoa kwa madai ya kujiandaa na michuano ya kimataifa. | 4 |
Na Mwandishi Wetu AKIWA na umri
wa miaka 27, Lauraa Teixeira, mkazi wa Amerika Kaskazini, kila anapoingia
kwenye hedhi, hukusanya damu yake na kupaka usoni, huku ile inayobaki akiichanganya
na maji kwa ajili ya kumwagilia mimea. Utaratibu huu
unaitwa ‘kupanda mbegu ya mwezi’ ambapo ni utamaduni ulioanzishwa na mababu
waliokuwa wakisherehekea damu ya mwezi na kuitambua kama ishara ya uzazi. Wanawake
wanaofuata utamaduni huu wana namna yao ya kusherehekea ‘miezi’ yao, ambayo
waliona kama ilikuwa na awamu, ambapo kila mzunguko ulikuwa na maana yake. Akizungumza
na BBC, Laura anasema alikuwa na maneno maalumu ya kumwagilia mimea, akiiambia:
“Samahani, nisamehe, ninakupenda na ninakushukuru.” Huwa anarudia maneno haya. Anasema: “Mimea huota na kuwa mizuri na kupokea virutubisho vingi.” Anasema kila anapofuta damu hiyo ya mwezi mwilini mwake, hufumba
macho yake na kujihisi mwenye shukrani na nguvu tena. Kwa Laura, mila hii ni huwaongezea nguvu wanawake. “Moja ya ubaguzi mkubwa kabisa ni mtazamo hasi wa jamii kuhusu
damu ya mwezi na jinsi ambavyo wanawake bado wanahisi aibu kuhusu hedhi yao,”
anasema. Naye Mwanasaikolojia, Mcheza dansi na mwandishi dansa, aliyeanzisha kampuni inayotekeleza mila hiyo – World Seed Your Moon Day, mwaka 2018, Morena Cardoso , anasema kupanda mwezi ni kitu rahisi mno, lakini chenye nguvu kubwa, kinachoponya na zoezi la kina kwa mwanamke. Mwaka jana, takribani watu 2,000 walipanda mbegu za damu yao ya
hedhi kwa pamoja katika maeneo ya umma. Morena anasema wazo la tukio hilo, ni kwamba damu ya hedhi si
sababu ya kumfanya mwanamke aone aibu, bali anapaswa kujivunia na humpa nguvu. ‘Kazi ya kiroho ya wanawake’ Kwa mujibu wa Morena, miongoni mwa tamaduni za wazawa Amerika
Kaskazini ikiwamo Mexico na Peru, damu ya hedhi ilikuwa ikimwagwa ardhini
kuifanya iwe yenye rutuba na yenye kumea mimea kwa wingi. Iliwakilisha muda wa ushirika na kazi ya kiroho ya wanawake, pia
ibada ya wanawake wanaojiandaa kuwa na heshima ya kike. Daniela Tonelli Manica, ambaye ni Mtaalam wa Historia ya Binadamu
katika Chuo Kikuu cha Brazil Unicamp, aliyefanyia utafiti suala la hedhi
miongoni mwa jamii kwa miaka 20, anasema katika jamii nyingine kuna mitazamo
hasi kuhusu damu ya hedhi. Anasema: “Damu ya hedhi huangaliwa kama utokwaji wa damu usio na
maana, ambao huwekwa katika kundi moja na kinyesi na mkojo – kitu ambacho
unamalizana nacho msalani, hakipaswi kuonekana machoni pa watu.” Katika miaka ya 1960s, vuguvugu la haki za wanawake lilitaka
kubadilisha mitazamo hii, likiwataka wanawake kuzungumzia zaidi juu ya miili
yao na kuheshimu maumbile yao. Wasanii walikuja baadae kuvumbua ishara ya damu ya hedhi kuelezea
maoni yao ya kisiasa kuhusu masuala ya mazingira, ngono na jinsia. Yatumika kumwagilia maua “Nilidhani ilikuwa ni haki na jambo sahihi kurejesha kwa dunia
kile inachotupatia,” anasema Renata, mwanamke ambaye hukusanya damu yake ya
hedhi bafuni na kuimwagilia kwenye mimea ya maua ya aliyoipanda kando ya nyumba
yake kwenye vyungu. Renata pia hupanda mimea ya minti ambayo haimwagilii na damu yake
ya hedhi na inaonekana kuwa ‘dhaifu’ utadhani ina ‘utapiamlo.’ Mara ya kwanza Renata mwenye umri wa miaka 43, alipopata hedhi,
akiwa na miaka kumi na zaidi, alikuwa ameambiwa kuwa: “Sasa wewe ni mwanamke
mchanga, utaanza kuvuja damu kila mwezi na watu hawapaswi kufahamu hilo.” Awali aliiona hedhi yake kama maudhi ya mara kwa mara na aliwaonea wivu wanaume ambao hawapati hedhi. Lakini sasa anaiona kama kitu ‘kitakatifu.’ Utafiti Utafiti wa dunia waliofanyiwa wanawake 1,500 walio na umri kati ya
miaka 14 hadi 24 unaonyesha ni kwa kiwango gani suala la hedhi bado ni mwiko
katika jamii nyingi. Kwa mujibu wa utafiti – ulioagizwa na Johnson & Johnson na
kufanyika katika nchi za Brazil, India, Afrika Kusini, Argentina na Ufilipino
– wanawake wanahisi aibu wanapoazima sodo (vitambaa vya hedhi), wanaoonekana
wakizihifadhi baada ya kuzitumia na hata kusimama kutoka kwenye viti vyao
wanapokuwa katika kipindi cha hedhi. Utata Lakini si kila mmoja yuko tayari kukubali mila ya kupanda mbegu ya
mwezi na hivyo ndivyo Laura alivyoibua mjadala mwezi uliopita baada ya kutuma
picha ya ‘selfie’ iliyoonyesha uso wake na kifua vikiwa vimepakwa damu ya
hedhi. “Nilikuwa na wafuasi 300 na nilifikiria utakuwa tu kama ujumbe wa
kawaida nilioutuma kwenye ukurasa wangu wa mtandao wa kijamii ili kumsaidia
mwanamke mwingine kuelewa mada,” anasema. Siku
nne baadae, alibaini kuwa alikuwa amedhalilishwa kwenye mtandao wa Instragram
ambapo vibonzo vya akaunti ya Instagram vilitumwa kumkejeli. Mchekeshaji mwenye utata nchini Brazil, Danilo Gentili, alifikiri
kuwa lilikuwa jambo la maana kutuma picha kwa wafuasi wake wa Instagram milioni
17, akisema: “damu ya hedhi ni ya kawaida, kitu ambacho hakikuwa cha kawaida ni
kuipaka kwenye uso wako.” Lakini utani wake haukuwafurahisha wengi, majibu 2,300 yakiwa ni
ya wale walioonyesha kutofurahishwa nao. Laura anasema kuwa yaliyotokea kuhusu ujumbe wake wa picha
yanathibitisha tu jinsi suala la hedhi lilivyo mwiko. “Watu wanafikiri kwamba ikiwa kama kitu si cha kawaida kwao, basi lazima kisikubalike. Wanafikiri wanaweza kujificha nyuma ya simu zao za mkononi na kutumia maneno ya chuki kumuumiza mtu fulani,” anasema na kuongeza. | 2 |
KOCHA Mkuu wa mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Patrick Aussems amewapoza wapenzi wa timu hiyo na kuwataka kutokata tamaa kwani bado wana nafasi ya kufanya vizuri katika Ligi ya Mabingwa wa Afrika licha ya kufungwa mabao 10 katika mechi mbili.Simba ilifungwa mabao 5-0 na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kabla ya kufungwa idadi kama hiyo ya magoli na Al Ahly ya Misri na hivyo kubaki na pointi tatu tu baada ya mechi tatu kufuatia kushinda 3-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika nyumbani dhidi ya JS Saoura ya Algeria.Akizungumza jijini Dar es Salaam, kocha huyo alisema katika mechi hizo mbili ametambua matatizo ya timu yao na anayafanyia kazi na timu hiyo itakuwa vizuri katika kipindi kifupi hata kabla ya kurudiana na Al Ahly Jumanne jijini Dar es Salaam.Alisema atahakikisha wachezaji wake wanakuwa vizuri na wanaondoka na pointi zote sita kutoka katika mechi mbili zilizobaki, ambazo watachezea kwenye Uwanja wa Taifa huku moja iliyobaki ndio itapigwa ugenini.Licha ya kupoteza michezo hiyo, lakini kocha huyo Mbelgiji bado ana matumaini ya kusonga mbele na kuwataka wachezaji wao kutokata tamaa na kujitokeza kwa wingi kuwashangilia siku hiyo.Alisema pamoja na kupoteza mechi mbili, lakini kundi lao bado liko wazi kwa timu zote kuweza kufuzu kwa hatua ya robo fainali kutokana na kutopishana kwa pointi nyingi.“ Niwaambie tuu mashabiki na wapenzi wa timu ya Simba waendelee kuiunga mkono timu yao na wasikatishwe tamaa baada ya kupoteza michezo miwili ugenini, bado tuna nafasi kwani michezo miwili ya hapa nyumbani naamini tutafanya vizuri,” alisema kocha huyo.Simba ambayo imepangwa kwenye Kundi D hadi sasa ni timu pekee iliyoruhusu idadi ya mabao mengi wamefikisha 10 katika mechi mbili walizocheza dhidi ya Al Ahly na Vita. Aussems aliwaomba mashabiki wa timu hiyo kuwa mstari kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa kuwasapoti ili kuwatia nguvu wachezaji wakati wakabiliana na timu bora kabisa barani Afrika. | 4 |
BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha kwa kishindo Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2019/2020.Bajeti hiyo ilipitishwa mjini hapa jana baada wabunge kupiga kura ya wazi ya kuitwa mbunge mmoja mmoja.Matokeo ya kura yalikuwa kama ifuatavyo: Wabunge waliopiga kura walikuwa 380 ambapo 12 hawakuwepo.Waliosema ‘Ndiyo’ ni 297 sawa na asilimia 78.2 na waliosema ‘Hapana’ ni 83 sawa na asilimia 21.8 Hotuba ya Bajeti iliwasilishwa wiki iliyopita na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango na mjadala wa bajeti hiyo ulichukua siku saba kabla kuhitimishwa jana.Awali, wakati Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mpango akijibu baadhi ya hoja za wabunge waliochangia, alisema kamwe saini yake haitoweza kutumika kusaini mikataba, itakayoiuza nchi hata kama atatukanwa vipi.Alisema ataendelea na msimamo wake huo, ikiwamo kutosaini mikataba mitatu ya miradi mikubwa inayohusu Zanzibar ambayo wafadhili wake wameweka masharti magumu ya dhamana ikiwemo kutaka kutumia mali za jeshi, mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), malikale, mali za kihistoria na za ubalozi kama dhamana ya mkopo.Wakati Dk Mpango akiweka msimamo huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Januari Makamba amemuomba Spika wa Bunge, Job Ndugai kuhakikisha Bunge hilo haliwi chanzo cha kuweka nyufa kwenye Muungano uliopo wa Tanzania na Zanzibar.Alitoa angalizo hilo kutokana na kauli za baadhi ya wabunge katika mjadala wa kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2019/20 dhidi ya Dk Mpango, zinazodai waziri huyo ana chuki na roho mbaya dhidi ya Zanzibar.Akihitimisha hoja ya kupitisha bajeti hiyo bungeni jana, Dk Mpango alielezea miradi hiyo mitatu na msimamo wake wa kuisaini hadi majadiliano yanayoendelea yatakapokamilika na ufumbuzi kupatikana, hata kama atatukanwa.Aliitaja miradi hiyo kuwa ni wa barabara ya Wete-Chakechake unaohusisha mkataba baina Benki ya Badea, Saudi Arabia na serikali kwa ajili ya mkopo wenye masharti nafuu wa kutekeleza mradi huo utakaogharimu dola za Marekani milioni 24.4.Alieleza kuwa katika mkopo huo, Benki ya Badea inatakiwa kutoa mkopo wa dola za Marekani milioni 10, Saudia dola za Marekani milioni 11 na Zanzibar itatoa dola za Marekani milioni 3 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo.Alitaja mradi mwingine ni wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Abeid Amani Karume (Terminal II) utakaogharimu dola za Marekani milioni 60 zitakazotolewa kama mkopo wa masharti nafuu na Benki ya Exim ya China.Alisema miradi yote hiyo miwili mpaka sasa hajaisaini kutokana na masharti magumu yaliyowekwa na wahisani hayo yanayohusisha kuweka dhamana ya mkopo watakaotoa mali kama vile za jeshi, BoT, malikale, mali za kihistoria na mali za balozi.Alisema katika mradi wa tatu wa ujenzi wa bandari ya Mpigaduri utakaogharimu dola za Marekani milioni 200 unaohusisha pia mkataba wa mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Exim, bado uko katika hatua ya uhakiki.Alisema miradi miwili yenye masharti magumu ya dhamana iko katika hatua ya majadiliano ya kidiplomasia ili kurekebisha tatizo hilo na masharti hayo yaondolewe.Alisema pamoja na kuonekana mbaya na kurushiwa kauli mbaya za kila aina, uamuzi wa kutosaini mikataba hiyo pia umeungwa mkono na kamati za kuipitia ambazo zote zinajumuisha wajumbe kutoka Bara na Zanzibar.Alifafanua kuwa mikataba yoyote itakayopitia mikononi mwake lazima ifanyiwe uhakiki ili kuepuka kuingia gharama kubwa zaidi zisizoendana na gharama za mradi.Awali, Januari alisikitishwa na kauli zilizotumiwa na wabunge wengi hasa wa Zanzibar dhidi ya Dk Mpango kuhusu miradi hiyo, na kusisitiza kuwa kauli hizo zimeleta na kuchangia hisia tofauti miongoni mwa jamii juu ya Muungano.Alisema alishangazwa kusikia kauli ya Mbunge wa Bumbwini, Muhammed Amour Muhammed (CUF), akiizungumzia bajeti ya Zanzibar huku akidai kuwa Waziri wa Fedha wa Zanzibar alimuelezea Dk Mpango kama ni mtu mwenye hasada, na mwenye roho mbaya kwa sababu hakusaini miradi hiyo ya maendeleo ya Zanzibar. | 3 |
Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Beng’i Issa amesema waratibu hao wana wajibu wa kuhakikisha wanatumia ujuzi walioupata kwa faida ya wananchi katika mikoa yao. Jumla ya waratibu 41 wa madawati ya uwezeshaji kutoka katika mikoa ya Ruvuma, Iringa, Njombe, Rukwa, Songwe na Mbeya walipatiwa mafunzo ya siku tatu jijini Mbeya.Mafunzo hayo yalimalizika mwishoni mwa wiki. “Tumewapatia mafunzo waratibu hawa wakafanye kazi kwa niaba ya baraza kutekeleza sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi,” alisema.Alisema mafunzo hayo yamelenga kuwapatia ufahamu wa kujua wajibu wao, kufanya kazi na jamii, kuibua fursa, kuwaonyesha fursa wananchi na kuwaunganisha na vyombo vya fedha na mifuko ya serikali kupata mikopo kuendeleza shughuli za kijasiriamali.Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa NEEC, mafanikio na changamoto zitakazojitokeza katika kanda hiyo zitatumika katika kuboresha kanda nyingine zilizobaki.Alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imeweka kipaumbele katika kuwawezesha wananchi kiuchumi hivyo kupitia waratibu hao wananchi watafikiwa kwa wingi na urahisi.Kaimu Katibu Tawala, mkoa wa Mbeya, Nyasebwa Chimagu alisema waratibu hao wamepatiwa dhamana kubwa na serikali hivyo wakatumike katika kupeleka elimu kwa wananchi juu ya uwezeshaji.Mratibu wa dawati la uwezeshaji, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Pelisius Kalikule alisema ameyapokea vizuri mafunzo hayo na amejipanga kwenda kufanya kazi aliyopewa na serikali. | 5 |
VIKOSI vya Usalama vya Kenya vimefanikiwa kutibua mpango wa kusafi risha binadamu uliokuwa umepangwa, ambapo mabinti zaidi ya 71 kutoka nchi za Uganda, Tanzania na Burundi walidakwa mjini hapa wakiwa katika harakati za kusafi rishwa kwenda ughaibuni.Mabinti hao walikamatwa kwenye Uwanja cha Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) katika jiji la Nairobi. Kwa mujibu wa vyombo vya Usalama vya Kenya, watu hao walikuwa wanapelekwa nchi za Uarabuni, hususan Oman. Miongoni mwa watu hao waliokamatwa, 59 ni raia wa Uganda wakiwa na hati za kusafiria za Uganda, saba wanatoka nchini Burundi na wengine watano waliobaki ni kutoka Tanzania.Maofisa katika JKIA walisema asilimia kubwa ya watu hao waliokuwa wakielekea Oman ni wanawake na inasemekana baadhi ya kazi walizokuwa wakiendea huko ni za ndani. Vyombo vya usalama vya nchi hiyo vilipata taarifa juu ya uwepo wa watu wenye hati za kusafiria zikiwa na mihuri bandia na vikafanikiwa kuwakamata na kinachofuata ni mashitaka na hatimaye kuwarudisha katika nchi zao.Idara ya Uhamiaji ya Kenya imesema kundi hilo la watu lilikuwa likitumia nyaraka bandia zisizo halali. Shirika la Habari la Kenya (KBC) liliripoti kuwa uchunguzi kubaini mashirika na taasisi zilizohusika katika kadhia hiyo ya usafirishaji wa watu unaendelea wakati utaratibu wa kuwasafirisha watu hao hadi katika nchi zao ukifanyika. Wiki iliyopita, wasichana 22 wa Uganda waliokolewa katika mikono ya maharamia wakisafirishwa kwenda Uarabuni.Waliokolewa katika mpaka wa Busia na Malaba nchini Kenya na kurudishwa nchini Uganda. Mratibu wa Kuzuia Usafirishaji wa Binadamu (CoPTIP) chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani Kamishna wa Polisi, Moses Binoga alisema wasichana hao 22 waliachiwa na Mamlaka za Kenya bila kushitakiwa kwa kuingia bila kibali nchini humo au kuwa na nyaraka batili za kusafiria.Alisema kwa wananchi wa Kenya ambao waliwahifadhi wahamiaji hao walishitakiwa kwa kuhifadhi wahamiaji haramu. Kabla ya kuondoka Kenya kuelekea Uarabuni, wasichana hao walihifadhiwa katika nyumba mbalimbali zilizokuwa chini ya wenyeji wao.Kwa mujibu wa maofisa nchini Kenya, kwa kila msichana au familia ya msichana ililipwa shilingi za Kenya milioni 1.5 ikiwa watafanikisha safari hiyo. Fedha hizo zinatumika pamoja na mambo mengine, kuwavusha wasichana hao hadi nchini Kenya ambapo watapanda ndege na kuelekea uarabuni. Asilimia kubwa ya wasichana wanaosafirishwa kwenda nchi za nje kutoka Uganda, DRC, Burundi na Tanzania wana umri wa miaka kati ya 16 hadi 25. | 3 |
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba Haji Manara amewataka mahasimu wao timu ya Yanga waje kwake awape mbinu ya namna ya kuujaza uwanja kama ambavyo hutokea katika klabu ya Simba hususan katika mechi za Kimataifa ngazi ya vilabu katika michuano ya CAF. Manara amesema hayo kufuatia klabu ya Yanga kupata fursa ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya CAF kuongeza idadi ya timu za Tanzania na kufika nne (mbili ligi ya Mabingwa, mbili Kombe la Shirikisho) kutokana na Simba kufika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa msimu huu uliomalizika. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameweka video akisema: “Kwanza waje kwangu wajifunze mbinu za kujaza uwanja kwa sababu zile si kwamba nafanya kwa kukurupuka tu, na next season (msimu ujao) nakuja na mbinu maalum sio tu za kujaza uwanja kwenye Champions League (Ligi ya Mabingwa) na kwenye ligi.” “Nina plan (mpango) wa kujaza uwanja kwenye kila mechi ya Simba ya Dar es Salaam kama tulivyokuwa tunajaza kwenye Champions League, na itakuwa this season (msimu huu) iwe tunachezaa na Mbao, ili mradi mechi ya Simba capacity (uwezo) elfu sitini, na tayari strategies (mikakati) hizo ninazo. Amewaambia Yanga waende wakasome kwake vinginevyo hawataweza kufanikisha kujaza uwanja kwani yeye hutumia mbinu nyingi kama vile kuwashirikisha wasanii. “Yanga waje kwangu wasome, hii ni University, ni chuo kamili, natoa degree (shahada), masters (shahada ya uzamili) na PhD (shahada ya uzamivu), waje kwangu wajifunze ” De la boss University imesajiliwa na Tume ya vyuo vikuu Duniani ( Tuvyodu) Karibuni sana 🙏 A post shared by Haji S. Manara (@hajismanara) on Jun 7, 2019 at 12:27pm PDT | 4 |
Serikali imeokoa Sh bilioni 51.2 baada ya kuboresha Taasisi ya Moyo ya Jakaya (JKCI) kwa kipindi cha miaka minne.Takwimu za mwaka 2015 za Shirika la Afya Dunia (WHO), zinaeleza zaidi ya watu milioni 17.7 walifariki kutokana na magonjwa ya moyo na mfumo wa damu.Hii ni sawa na theluthi ya vifo vyote, vinavyotokana na ugonjwa wa moyo na mishipa ya damu, vinavyotokea kwenye nchi zenye uchumi wa chini na ule wa kati.Mara nyingi magonjwa ya moyo yanaambatana na mishipa ya damu kuwa na tatizo, ambapo moyo hushindwa kufanya kazi, moyo hutegemea damu ambayo hubeba oxygen, madini, vitamin, kinga ya mwili, joto, homoni na vingine vingi.Kufuatia hali hiyo, HabariLeo ilifanya mahojiano maalum na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi ambaye amesema kuanzishwa kwa taasisi hiyo, wameweza kuokoa maisha ya watu wengi ndani na nje ya nchi.Hali hiyo ni tofauti na siku za nyuma ambapoo serikali ilipeleka nje wagonjwa 200 kila mwaka kwa ajili ya matibabu ya moyo.“Magonjwa ya moyo ndio ilikuwa namba moja kwa kupeleka wagonjwa nje, serikali ilikuwa ikipeleka wagonjwa 400 kwa mwaka, kati yao wagonjwa 200 ni wa moyo… wakati Rais Magufuli anaingia madarakani alikuta kuna deni la mabilioni kwa sababu ya kupeleka watu India,” alisema.Profesa Janabi amesema mgonjwa mmoja, alikuwa anapelekwa nje na kutibiwa kwa gharama ya dola 30,000 sawa na shilingi milioni 60.Kwa maana hiyo, kwa wagonjwa 200 kwa kipindi cha miaka minne, wangetibiwa kwa gharama ya shilingi bilioni 51.2.Alisema kabla ya 2015, Tanzania iliongoza kwa kupeleka wagonjwa nchini India kwa asilimia 90, idadi ambayo ni kubwa. Hata hivyo, tangu kipindi hicho mpaka mwaka huu, wamepunguza idadi ya wagonjwa kuwapeleka wagonjwa nje kwa asilimia 90.“Tuna namba kubwa ya watu tunaowafanyia upasuaji humu ndani, kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2015 mwishoni mpaka mwaka jana wa 2018 tumepasua wagonjwa 3,000. Kama serikali bado ingekuwa na utaratubu wa kupeleka wagonjwa 200 kwa mwaka wa moyo kwa miaka mitano ilikuwa ni wagonjwa 1,000 sasa kwa wagonjwa 3,000 ingetuchukua miaka 15 kuwamaliza wagonjwa wote. Wagonjwa 8,000 hatujawafanyia upasuaji, wanatibiwa kwa vidonge na dripu, wangeweza kupelekwa India na kufika kule wangeambiwa ni wa vidonge, na dripu mgonjwa mmoja tulikuwa tunampeleka kwa dola 30,000 sawa na shilingi milioni 60,” amesema Profesa Janabi.Alisema taasisi hiyo inamilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na ilianzishwa Septemba 5, mwaka 2015 kwa thamani ya Sh bilioni 26, huku serikali ya China ikitoa Sh bilion 16 na serikali ya Tanzania Sh bilioni 10.Kwamba kwa miaka minne wameweza kuwaona wagonjwa 291,800 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani pamoja na nchi jirani, ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Malawi, Ethiopia, Zambia, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda na Visiwa vya Comoro.Alisema tangu taasisi ya JKCI ilipoanzishwa, wana mkataba na Malawi na Rwanda, ambapo wamewaokoa wagonjwa 25 baada ya watalaamu wa JKCI kuweka kambi Kigali, Rwanda. Awali awali Rwanda walikuwa wakipeleka wagonjwa India.Pia alisema taasisi hiyo imeweza kuokoa maisha ya watanzania ambao wametibiwa na hivi sasa wanaendelea na majukumu yao ya kazi za kila siku.Kwa kwa kipindi cha miaka minne, walilazwa wagonjwa 14,645, upasuaji wa bila kufungua kifua kwa kutumia tundu dogo kwa mtambo wa Cathlab umefanyika kwa wagonjwa 3,180 na upasuaji wa kufungua kifua na kusimamisha moyo kwa wagonjwa 1,627. Janabi alisema kama wagonjwa wote hao, waliofanyiwa upasuaji wangetibiwa nje ya nchi serikali ingetumia zaidi ya Sh bilioni 144.Kwa wagonjwa hao kutibiwa hapa nchini, matibabu yao yamegharimu Sh bilioni 72, fedha ambazo zimelipwa kupitia bima zao mbalimbali za matibu, misaada ya wafadhili mbalimbali wa nje, wagonjwa wenyewe kujilipia na Serikali kugharamia matibabu ya wagonjwa wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za matibabu. Gharama ya kumtibu mgonjwa mmoja nchini ni zaidi ya Sh milioni 29.Vifaa vya KisasaKaimu Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa JKCI, Melkiory Sallema alisema kwa kipindi cha miaka minne taasisi hiyo imeweza kununua mashine za kisasa za matibabu ya moyo, zikiwemo mashine za kuchunguza jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiograph - ECHO), mashine ya kuchunguza umeme wa moyo unavyofanya kazi (Electrocardiogram-ECG), mashine za Ventilators, Cardiac monitor, Test gears, mashine ya X - Ray.Thamani ya mashine zote hizo ni Sh 2,178,863,009. Alisema wadau wao kutoka taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart - SACH) ya Israel, iliwapatia mashine ya kuchunguza jinsi moyo unavyofanya kazi yenye thamani ya Sh 110,898,000 kwa ajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI.Alisema ndani ya miaka minne, taasisi hiyo imefanikiwa pia kufungua maabara ya kisasa kwa ajili ya kuchunguza magonjwa mbalimbali yanayoambatana na magonjwa ya moyo kama vile uchunguzi wa ini, figo, malaria, sukari, homoni na uchunguzi wa damu mwilini.Paja/Mkono kuzibua mishipaProfesa Janabi akifafanua kuhusu mtambo wa Cath lab ambao umenunuliwa kwa gharama ya Sh bilioni tano, alisema matibabu yake wanatumia mshipa wa paja au mkono kuangalia kama moyo umeziba.“Tunatumia waya zetu mpaka kwenye moyo kujua umeziba kwa asilimia ngapi, tunaingia kitu kama vyuma lakini sio vyuma hasa vyetu ambayo kimoja ni gharama shilingi 3,000,000, tunaingiza na kuzibua kupitia mshipa wa paja au mkono… kuna tunaowawekea betri, tunapasua juu ya ziwa na tunaweka mashine karibu na bega, tunaingia na waya, zile waya ndio zinakuwa zinatuongoza, upasuaji huu wa tundu ndogo unakuja saa 12 asubuhi, jioni tunakuruhusu kuondoka,”alisemaMfumo wa umemeProfesa Janabi alisema moyo una mfumo, ambao kama haufanyi kazi sawa sawa, ndio wanamuwekewa ‘pacemaker’ ambao ni mfumo wa umeme uliotengenezwa na binadamu ili kupeleka umeme kwenye moyo.Wodi Maalum ya WatotoMkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo kwa Watoto, Dk Sulende Kubhoja alisema kuwepo kwa Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) kwa watoto, kumeongeza idadi ya watoto wanaofanyiwa upasuaji kutoka 20 hadi 40 kwa mwezi, hivyo kupunguza muda wa kusubiri kupata matibabu ya upasuaji wa moyo. “Jengo hili lina vyumba vya kliniki vinne, chumba cha wagonjwa waliopo ICU chenye vitanda nane na wodi yenye vitanda 33.Tumeweza kutimiza mkakati wetu wa kupunguza msongamano wa wagonjwa na kuwafikia kimatibabu watoto wengi zaidi,” alisema Dk Kubhoja.Viongozi waikimbiliaProfesa Janabi alisema uwekezaji uliofanywa na serikali ndani ya taasisi hiyo umelipa; na viongozi kutoka ndani na nje ya nchi, wanaenda kutibiwa hapo.“Viongozi mbali mbali wa serikali na dini wanatibiwa hapa,” alisemaChangamotoAlisema licha ya Rais John Magufuli kuwapa ghorofa moja Muhimbili, ambayo imefanyiwa matengenezo na ndio imekuwa wodi maalum ya watoto, bado wana changamoto ya vitanda.Profesa Janabi alisema mpaka sasa wana vitanda 140, ambapo vitanda 100 vipo jengo la JKCI na 40 vipo jengo la watoto kwenye wadi maalum ya watoto wenye matatizo ya moyo.“Nchi yetu na nchi za jirani zote zinategemea hapa, hii ndio hospitali pekee kubwa ya moyo Afrika Mashariki na Kati, nyingine zote zina vitengo vya moyo, licha ya hatua kubwa tuliopiga kama taasisi lakini bado tunahitaji kuongeza vitanda zaidi,” alisema.JKCI nyingine MloganzilaAlisema wapo mbioni kuongeza jengo la pili la taasisi hiyo ya moyo Muhimbili Mloganzila, ambalo litakuwa kubwa kuliko lililopo sasa.Alisema tayari wamechagua eneo Mloganzila, lenye ukubwa wa mita za mraba 30,000 na litaanza kujengwa rasmi mwaka 2020 na China na serikali watanunua vifaa.Alisema tayari wamewapeleka mafunzo ya moyo wauguzi na madaktari 36 nje ya nchi na watakaporeja tayari jengo hilo la JKCI Mloganzila litakuwa limekamilika.Wagonjwa waipa tanoBenedictor Maina ambaye ana umri wa miaka 101, aliyefanyiwa upasuaji na kuwekewa kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo ili yawe sawa, alikuwa akipata maumivu makali sehemu za moyo, kuanguka, kupoteza fahamu na kushindwa kutembea.Lakini, baada ya kufanyiwa upasuaji huo, hali yake imebadilika na maumivu yamekwisha. Mkazi wa DRC, Nura Babu alisema alipata rufaa kutoka Burundi ya kwenda kutibiwa Uganda na baada ya kufika Uganda, hakuridhika na huduma ya matibabu ya moyo, iliyokuwa inatolewa huko. Alipewa ushauri na daktari wa kuja nchini Tanzania. | 3 |
MIPAKA ya Tanzania na nchi za Kenya, Uganda na Burundi imeanza kuimarishwa katika hatua mbalimbali ili kufikia lengo la serikali kuhakikisha ifikapo mwaka 2022 uimarishaji wa mipaka hiyo kuwa imekamilika.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alibainisha hayo katika hotuba yake ya bajeti aliyoitoa hivi karibuni na kueleza kuwa katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 wizara iliahidi kuendelea na uimarishaji wa mpaka wa Tanzania na Uganda, Tanzania na Burundi, Tanzania na Kenya na Tanzania na Zambia.Aidha, uimarishaji huo unakwenda sambamba na katika mipaka ya nchi ndani ya Ziwa Tanganyika na nchi za Burundi, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).Lukuvi alisema ununuzi wa vifaa vya ujenzi wa alama za katikati za mpaka umefanyika, maandalizi ya kuweka alama za mpaka yamefanyika kupitia kikao cha makatibu wakuu wanaohusika na mpaka wa Tanzania na Uganda kilichofanyika Aprili mwaka huu mjini Bukoba,mkoani Kagera.Alisema mpaka ndani ya maji katika Ziwa Victoria kati ya Tanzania na Uganda wenye urefu wa kilometa 246 haujaanza kuimarishwa.Aliongeza kuwa mpaka wa Tanzania na Kenya wenye urefu wa kilometa 819.7 kati ya hizo kilometa 760 za nchi kavu na kilometa 59.7 ziko ndani ya maji katika Ziwa Victoria. Uimarishaji wa mpaka huo unaelezwa kujumuisha utengenezaji wa ramani za msingi, kupima kipande cha mpaka na kusimika alama za ardhini.Alisema kilometa 172 kati ya 760 za nchi kavu ziliimarishwa kufikia Juni mwaka jana na kwa mwaka wa fedha 2018/2019 mpaka mei mwaka huu kilometa 128 kutoka Ziwa Natron hadi Namanga zimekaguliwa ili kubaini mahitaji halisi.Waziri alisema mpaka kati ya Tanzania na Zambia ni kilometa 345 ambapo sekta ya nchi kavu ina kilometa 289 na ndani ya maji ina urefu wa kilometa 56 maandalizi yanaendelea kwa ajili ya kuimarisha mpaka huo kwa makubaliano na Serikali ya Zambia ifikapo mwezi huu. | 3 |
BARCELONA, HISPANIA HATIMAYE mshambuliaji hatari wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi, amefanikiwa kumfunga mabao kwa mara ya kwanza mlinda mlango wa klabu ya Juventus na timu ya Taifa ya Italia, Gianluigi Buffon, kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya huku Barcelona ikishinda mabao 3-0. Mchezo huo ambao ulipigwa juzi kwenye Uwanja wa Camp Nou, hatua ya makundi, Messi aliweza kuandika historia mpya ya kumfunga mlinda mlango huyo ambaye amekuwa akipata wakati mgumu kila anapokutana naye. Messi alifunga bao lake la kwanza katika dakika ya 39 kipindi cha kwanza kabla ya kipindi cha pili kuongeza bao lake la pili huku lingine likiwekwa wavuni na Ivan Rakitic. Buffon mwenye umri wa miaka 39, katika michezo mitatu ya Ligi ya Mabingwa waliyokutana na Barcelona, aliwahi kusema hawezi kufungwa na mchezaji huyo na atahakikisha anafanya hivyo kila wanapokutana, lakini juzi alishindwa kumzuia na kufanikiwa kuivunja historia hiyo. Ilikuwa miaka 12 tangu Messi aanze kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya na kukutana na mlinda mlango huyo. Kocha wa Juventus, Massimiliano Allegri, amedai alijua lazima apoteze mchezo huo kutokana na ubora wa wapinzani wao. “Nawajua vizuri Barcelona, nadhani hii itakuwa mara ya 12 kukutana na timu hiyo, nimekuwa nikiujua uwezo wa Messi, siku zote ninawaambia wachezaji wangu kuwa mchezaji huyo ana uwezo tofauti lazima wawe makini. “Bila ya kujali kuondoka kwa Neymar, lakini Barcelona bado ni klabu bora duniani kama ilivyo kwa Real Madrid, kukutana na timu hizo mara tatu bila ya kukufunga inakuwa jambo la historia. “Ninaamini Barcelona na Real Madrid ni wababe wa Ligi ya Mabingwa, lakini kwa upande wetu naweza kusema huu ni mwanzo bado tuna nafasi ya kufanya vizuri,” alisema Allegri. Mbali na mchezo huo wa Barcelona dhidi ya Juventus, mitanange mingine iliopigwa juzi ni pamoja na Chelsea ikishinda mabao 6-0 dhidi ya Qarabag FK, Sporting ikishinda mabao 3-2 dhidi ya Olympiacos, CSKA Moscow ikiichapa Benfica 2-1, AS Roma wakitoka bila kufungana dhidi ya Atletico Madrid na Man United ikishinda mabao 3-0 dhidi ya FC Basel, PSG wakishinda 5-0 dhidi ya Celtic na Bayern Munich wakishinda 3-0 dhidi ya Anderlecht. | 2 |
Matokeo hayo yanaifanya Yanga izidi kujichimbia kileleni ikiwa na pointi 46 huku bingwa mtetezi Azam ikiwa nafasi ya pili na pointi 37 na nafasi ya tatu inashikwa na Simba yenye pointi 35.Yanga inahitaji ushindi wa mechi mbili kutangaza ubingwa kwani itafikisha pointi 58 ambazo hazitafikiwa na Azam hata akishinda mechi zote sita zilizosalia.Yanga ilianza mechi ya jana kwa kasi huku washambuliaji wake wakionekana wenye uchu wa mabao kama ilivyokuwa Jumatano iliyopita ambapo iliifunga Coastal Union ya Tanga mabao 8-0.Wawakilishi hao wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa, waliandika bao la kwanza katika dakika ya 18 mfungaji akiwa Kpah Sherman aliyefunga kwa shuti kali ndani ya eneo la hatari baada ya mpira uliokuwa umepigwa na Amissi Tambwe kuwababatiza mabeki wa Mbeya City.Bao hilo liliongeza kasi ya mchezo kwa timu zote mbili lakini Salum Telela aliifungia Yanga bao la pili katika dakika ya 37 baada ya kupiga shuti kali lilowababatiza mabeki wa Mbeya City na kumpoteza kipa Hanington Kalyesubula.Mbeya City ambao Jumatano iliyopita walitoka sare ya 1-1 na Azam FC kwenye uwanja wa Azam Complex, walikuja juu na kufanikiwa kupata bao la kufutia machozi dakika ya 39, akiunganisha pasi ya Raphael Alpha.Dakika nne baada ya kuanza kipindi cha pili nahodha wa Yanga, Nadir Haroub aliifungia timu yake bao la tatu akiunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu ndogo uliokuwa umepigwa na Haruna Niyonzima dakika ya 49.Mbeya City inayoshiriki ligi kwa msimu wa pili, ililazimika kucheza pungufu baada ya mwamuzi Mathew Akrama wa Mwanza kumtoa kwa kadi nyekundu Felix kwa kumchezea rafu Telela katika dakika ya 53.Rafu hiyo ilimfanya Telela kushindwa kuendelea na kulazimika kutolewa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Hassan Dilunga katika dakika ya 61.Dakika ya 21, Sherman alikosa bao baada ya shuti lake kupanguliwa na kipa wa Mbeya City, Kalyesubula. | 4 |
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019 kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza. “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake. | 5 |
Jessca Nangawe GWIJI wa muziki wa dansi nchini, Asha Baraka ambaye alikua
Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta, ametaja sababu zilizomfanya kukaa
pembeni. Asha Baraka ambaye ameiongoza bendi hiyo kwa zaidi ya miaka
20, alisema ameamua kumuachia majukumu yake Luiza Mbutu kutokana kuwa na mambo mengi. Akizungumza na MTANZANIA jana alipotembelea ofisi za New
Habari Ltd, zilizopo Sinza Kijiweni alisema wameamua kubadili muundo mzima wa
bendi hiyo kwa kuhakikisha inafanya kazi kisomi zaidi huku akiamini Luiza
atatosha kuvaa viatu vyake akisaidiana na Msafiri Diof pamoja na Chaz Baba. Alisema kwa sasa anakabiliwa na majukumu ndani ya klabu ya
Simba, kujiandaa na kampeni za uchaguzi mkuu kumsapoti rais wa awamu ya tano, kukuza
vipaji vya wasanii chipukizi pamoja na kuwa mshauri ndani ya bendi hiyo. “Nimeachia madaraka ndani ya Twanga lakini haimaanishi
ninaondoka, nitabaki kuwa mshauri, hii inatokana na kubanwa na majukumu mengine
ya kazi na naamini Luiza Mbutu atatosha sana kuva viatu vyangu,”Alisema. Aliongeza kwa kuwataka mashabiki wa bendi hiyo kumwamini
Luiza kwani amekaa na bendi hiyo kwa miaka 20 na ana uzoefu mkubwa wa kuiongoza
na kuifikisha mbali hata zaidi ya yeye alipoifikisha. Kwa upande mwingine Asha ameiomba Serikali kuhakikisha
inawatengea wasanii nafasi za kumbi za burudani ili kuwapa motisha na kurudisha
uhai wa bendi nyingi ambazo zimeonekana kupotea kutokana na kukosa sapoti. | 1 |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.