text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
Na ADAM MKWEPU-DAR ES SALAAM WADAU mbalimbali wa mchezo wa soka nchini wameitaka Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kutafakari upya vigezo wanavyotumia kumpata kocha sahihi wa kuifundisha timu ya soka ya Taifa. Hatua hiyo inatokana na matokeo mabaya ya timu ya Kilimanjaro Stars waliyopata katika michuano ya Kombe la Cecafa, yanayoendelea nchini Kenya. Kilimanjaro wameondolewa katika michuano hiyo baada ya kufungwa bao 1-0 na wenyeji, Kenya na kumaliza nafasi ya mwisho kwenye kundi A, wakiwa na pointi moja katika mechi nne walizocheza, wakifungwa mechi tatu na kwenda suluhu mchezo mmoja, huku wakifunga mabao mawili pekee katika michezo yote. Wakizungumza kwa wakati tofauti na MTANZANIA jana, wadau hao walisema Kamati ya Ufundi iweke wazi vigezo vilivyotumika kumteua kocha wa timu, kutokana na ukakasi uliopo, kwa kile kilichotokea kwenye michuano ya Cecafa Kenya. Kocha wa zamani wa timu ya Mbeya City na Yanga, Juma Mwambusi, alisema wasiwasi wake upo kwa wahusika waliomteua kocha huyo ili kuifundisha timu ya taifa. “Mimi ni Mtanzania kama wengine, naumia nikiona hali hii kama ilivyo kwa wengine, TFF ndio wenye jukumu la kumteua kocha, ila sijui kama walitumia vigezo sahihi kumpata Ninje. “Timu ya taifa si ya kufanyia majaribio, hata kama alikuwa mchezaji wa zamani na alisomea ukocha je, anafahamu mazingira ya hapa nchini? Aliwahi kufundisha timu yoyote na alitambua utayari wa wachezaji aliokabidhiwa?” alihoji Mwambusi. Mchezaji wa zamani wa Yanga na mchambuzi wa soka nchini, Ally Mayay, alisema waliomteua Ninje kuwa kocha wa timu ya taifa walisahau mahitaji ya Watanzania. “Hatukwenda Kenya kujifunza, badala yake tulitaka kushinda taji kwa kuwa  michuano ya Cecafa tunaimudu, tulifanya hivyo katika michuano ya mwaka 2010 na tulikuwa na uwezo wa kufanya tena mwaka huu, ndiyo maana kuna wachezaji wazoefu,” alisema Mayay. Kocha wa timu ya Dodoma FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio‘, aliishauri Kamati ya Ufundi ya TFF kutojali zaidi vyeti, badala yake wajikite kwenye ubora wa kocha. “Kocha bora Tanzania kwa sasa ni Meck Maxime, lakini TFF hawakuliona hilo, wao wakavutiwa na kocha anayejua kuzungumza lugha ya Kiingereza. “Kwa hili TFF na kamati husika wanatakiwa wajitafakari upya na nitakwenda kumweleza Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi, bila kumwonea haya kwamba uteuzi wake haukuwa sahihi,” alisema Julio. Kocha wa Kagera Sugar, Meck Maxime, alisema licha ya TFF kuwa na viongozi wanaofahamu mpira, wanatakiwa kujifunza kutokana na makosa, kabla ya kuwapa makocha majukumu ya kitaifa. “Wahusika wanatakiwa kujifunza na kubadilika, makocha wanaofahamu mazingara ya hapa nyumbani wapo wengi, hao ndio waliotakiwa kutumiwa na si vinginevyo,” alisema Maxime.   Kocha Ammy Ninje  ana leseni ya ukocha daraja A la Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) na tayari ameshawaomba radhi Watanzania,  akiahidi kutengeneza kikosi bora   kitakachoshiriki michuano ijayo. Akizungumza baada ya kuondolewa katika michuano hiyo, Ninje alisema mpango wake ulikuwa kurudi na kombe hilo nchini, ila kutokana na matokeo hayo anarejea kujipanga upya michuano ijayo. “Tatizo lipo kwa wachezaji namna tulivyowalea, hawakuwa na kasi, ukiacha mchezo dhidi ya Zanzibar, iliyobaki yote tulicheza vizuri, ingawa hatukupata matokeo mazuri. “Tunaomba Watanzania watusamehe kwa kuwaangusha, kwani halikuwa lengo letu, tunawaomba waendelee kuisapoti timu yao na tunawaahidi kuboresha tulipokosea,” alisema Ninje.
4
*TFF watuma salamu za rambirambi NFF NA BADI MCHOMOLO, DAR ES SALAAM KOCHA wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Boniface Mkwasa, amedai kuguswa na kifo cha aliyekuwa kocha wa timu ya Taifa ya Nigeria (Super Eagles), Stephen Keshi, ambaye amefariki jana mjini Benin nchini Nigeria. Mkwasa amedai kwamba alikuwa anajifunza mengi kutoka kwa kocha huyo ambaye alifanya makubwa kwa taifa lake tangu akiwa mchezaji hadi nafasi ya ukocha. “Kifo cha Keshi kimemgusa kila mmoja mwana familia ya soka hasa kwa upande wa barani Afrika, alikuwa kocha wa mfano kwa makocha wengi Afrika kwa kuwa aliweza kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa Afrika akiwa kama mchezaji. “Hata hivyo, wakati anaifundisha timu hiyo mwaka 2013 aliipatia ubingwa huo kwa mara ya pili, hivyo ni historia kubwa ambayo ameiacha katika historia ya soka nchini humo. “Kwa upande wangu nikiwa kama kocha mzawa wa Taifa Stars nilikuwa najifunza mengi kupitia yeye, hasa kwa kujipa moyo wa kuisaidia timu yangu ya Taifa nikiwa kama mzawa, pengo hili ninaamini haliwezi kuzibwa na yeyote. “Ninaungana na familia ya wanasoka wote Afrika kwa ujumla katika kipindi hiki kigumu kwa kumpoteza kiongozi huyo bora katika soka,” alisema Mkwasa. Kwa upande wa Frederick Mwakalebela, alisema: “Keshi ni kocha ambaye ameleta utamaduni wa nchi mbalimbali kuwaamini makocha wazalendo na kuwapa timu za Taifa, tutamkumbuka kwa misimamo yake na mafanikio aliyowapatia Wanigeria,” alisema Mwakalebela. Keshi amepoteza maisha ghafla huku akiwa na umri wa miaka 54, kwa mujibu wa wanafamilia na marafiki zake wa karibu, Keshi hakuonesha dalili zozote za kuumwa, ila inadaiwa kwamba kocha huyo amepoteza maisha kutokana na msongo wa mawazo kwa kumpoteza mke wake ambaye alifariki mwaka jana kutokana na kusumbuliwa na saratani. Keshi amekuwa kocha pekee mzawa kutwaa taji la Mataifa ya Afrika akiwa kama mchezaji na baadaye akiwa kocha, mbali na kuifundisha Super Eagles, aliwahi kuifundisha Togo na Mali. Alianza kuichezea timu ya Taifa akiwa na umri wa miaka 20 kuanzia mwaka 1982 hadi 1994, akiwa nahodha wa timu hiyo ambapo alikuwa anacheza nafasi ya ulinzi. Taifa Stars inatarajia kukutana na Super Eagles kwenye michuano ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika, mchezo huo unatarajiwa kupigwa Septemba 2 mwaka huu nchini Nigeria, huku wenyeji hao wakiwa chini ya kocha wao, Daniel Amokach. Hata hivyo, Stars itacheza na Nigeria kwa kukamilisha ratiba yake kwa kuwa tayari ndoto za kufuzu zimeyeyuka huku kundi hilo likiongozwa na Misri, ambao tayari wana pointi 10 wakifuatiwa na Nigeria wenye pointi 2, huku Tanzania ikiwa na pointi 1. Shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF), linaungana na wanasoka wote katika kuomboleza kifo cha nyota huyo wa zamani wa Nigeria, Keshi ambapo Rais Jamal Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Nigeria (NFF), Amaju Pinnick, familia ya marehemu Keshi pamoja na ndugu, jamaa, marafiki walioguswa na msiba wa gwiji huyo. Katika rambirambi ambazo zimefika pia katika Ofisi za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Rais Malinzi amesema kuwa japokuwa Keshi ametangulia mbele za haki, mchango wake kwenye mpira wa miguu hautasahaulika kwani atabaki kuwa alama ya maendeleo ya mchezo wa soka.
4
WADAU wa uzalishaji wa mvinyo nchini pamoja na watumiaji wa kinywaji hicho wanatarajia kusherehekea pamoja Siku ya Wapendanao kwa kujumuika katika hafl a ya maalumu iliyopewa jina la ‘Mkeka na Mvinyo’.Hafla hiyo ya kipekee inatarajiwa kufanyika usiku wa Februari 14 ambayo ni ‘Siku ya Wapendano’ katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam, na kuwahusisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi wa kawaida.Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa hafla hiyo kutoka Kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Caroline Kirwanda amesema mbali na kuwakutanisha wadau muhimu wa kinywaji hicho, hafla hiyo inalenga kutoa fursa kwa watumiaji kufurahia vinywaji tofauti vya aina hiyo vinavyozalishwa nchini wakiwa wamekaa kwenye mikeka.“Pamoja na kutoa fursa kwa watumiaji wa mvinyo siku hiyo kufurahia pamoja na wapendwa wao, usiku wa Mkeka na Mvinyo unalenga kuunga mkono jitihada za serikali katika kutangaza utalii na kukuza viwanda vya ndani kupitia uhamasishaji wa matumizi ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ikiwemo aina tofauti ya mvinyo bora kabisa unaozalishwa hapa nchini,” alisema Kirwanda.“Upekee wa hafla hii unaanzia kwenye jina lake ‘Mkeka na Mvinyo’. Hivyo basi itahusisha matumizi ya mikeka ambayo wageni wetu watapata fursa ya kuketi kwenye mikeka huku wakifurahi mvinyo bora unaozalishwa hapa nchini pamoja na nyama choma kadili ya matakwa yao,” aliongeza.Aliwataja baadhi ya wadau muhimu katika kufanikisha hafla hiyo kuwa ni Hoteli ya White Sands, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), GS 1, na Kampuni ya Magazeti ya Serikali, wazalishaji wa Daily News, Habari Leo na SpotiLeo.Kirwanda aliongeza kuwa hafla hiyo ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo utakaozinduliwa hivi karibuni unaolenga kutangaza utalii wa ndani pamoja kuvumbua fursa mbalimbali za kibiashara ndani ya nchini kwa lengo la kukuza uchumi unaofahamika kwa jina la ‘Mpango wa Kukuza Utalii wa Ndani (DTPI).“Tunahitaji kuhamasisha zaidi matumizi ya bidhaa za ndani ili kukuza uchumi wetu kama Taifa,” aliongeza Kirwanda huku akitaja baadhi ya maeneo ambayo tiketi za hafla hiyo zinapatikana kuwa ni Hoteli ya White Sands na Shamo Tower, Mbezi Beach.Amesema tofauti na mtu mmoja mmoja au kwa wale ambao watakuwa na wapendwa wao, Mkeka na Mvinyo inatoa fursa kwa mashirika na taasisi kufurahia pamoja katika dhana nzima ya kuonesha upendo, shukrani na pongezi baina yao na wadau wao katika shughuli zao za kila siku huku wakifurahia mvinyo na chakula kizuri.“Ifahamike kwamba Siku ya Wapendanao sio kwa ajili ya wale wenye mahusiano ya kimapenzi tu, bali pia inaweza kutumiwa na mashirika au taasisi mbalimbali, lengo likiwa ni kuonesha upendo, shukrani na pongezi kwa wafanyakazi na wadau mbalimbali wanaoshirikiana nao katika shughuli zao za kila siku,” amesema.Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Januarius Maganga amesema kampuni hiyo imeamua kuunga mkono mpango huo kutokana na kuguswa kwake na namna unavyolenga kuchochea harakati za masoko kwa bidhaa za ndani sambamba na kuunga mkono ajenda ya serikali ya uchumi wa viwanda.Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa TTB, Geoffrey Tengeneza amesema kupitia mpango huo, mbali na kutangaza utalii wa fukwe, pia utatangaza utalii wa asili kwa kuwa utahusisha mvinyo unaozalishwa nchini huku watumiaji wakiwa wameketi kwenye mikeka ya asili.
3
PATRICIA KIMELEMETA NA CHRISTINA GAULUHANGA-DAR ES SALAAM KIONGOZI wa Chama cha ACT- Wazalendo , Zitto Kabwe amelitaka Jeshi la Polisi limshtaki mahakamani ili madai yake dhidi ya sheria ya takwimu yapate tafasiri ya kisheria. Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Kituo cha Polisi cha kushughulikia makosa ya uhalifu wa kimtandao eneo la Kamata jijini Dar es Salaam, alisema anataka kesi hiyo ipelekwe mahakamani ili tafasiri sahihi ya kisheria kuhusu masuala ya takwimu itolewe. “Sheria ya takwimu ni miongoni mwa sheria zilizokuwa zinapigiwa kelele na wabunge kabla ya kupitishwa lakini Serikali ilifanya haraka kuipitisha huku ikiwa na upungufu katika baadhi ya vipengele. Upungufu huo unanyima uhuru wa kutoa taarifa,” alisema Zitto. Alisema ni wakati mwafaka kwa Polisi kuifikisha kesi yake hiyo mahakamani ili mgongano uliopo uweze kupatiwa majibu ya kisheria na chombo hicho. “Itakuwa ni kesi ya kwanza ya takwimu kufikishwa mahakamani tangu sheria hii ilipopitishwa na Bunge na hicho ndicho ninachokitaka kwa sababu kesi za takwimu haziwezi kumalizika kinyemela kwani zinaweza kuleta utatanishi,” alisema Zitto. Awali kabla ya kuhojiwa kuhusu takwimu alizozitoa zikipingana na za serikali kuhusu ukuaji wa uchumi, Zitto alisema ACT  kilipanga kufungua kesi ya kuondoa vipengele vinavyokandamiza uhuru wa kutoa taarifa na maoni katika sheria ya takwimu. Alisema hilo likifanakiwa litatoa tafasiri ya kisheria na kuondoa vipengele vinavyokandamiza utoaji wa taarifa. Kabla ya kufika Kituo cha Polisi Kamata, Zitto alikwenda Kituo cha Polisi Chang’ombe kusikiliza tuhuma anazoelekezewa kuwa alitoa maneno ya uchochezi katika baadhi ya mikutano yake ya kisiasa. Zitto aliwasili katika kituo hicho saa 10:37  na kutoka saa 4:47 baada ya kutakiwa aripoti tena Novemba 17, 2017. Alisema polisi walimweleza faili lake bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hivyo arudi Novemba 17. “Nimefika kituoni kuitikia wito wa polisi kama nilivyoambiwa wiki iliyopita lakini wamesema faili langu lipo kwa DPP ambaye analipitia kabla hajaamua kama napelekwa mahakamani au la,” alisema Zitto. Jana viongozi wa ngazi za juu wa ACT- Wazalendo, walihojiwa na Polisi wa Kitengo cha Makosa ya Uhalifu wa Kimtandao na Takwimu kuhusu takwimu za uchumi zilizotolewa na Zitto. Waliohojiwa ni Kaimu Mwenyekiti, Yeremiah Maganja, Katibu Mkuu, Doroth Semu na Mkurugenzi wa Ulinzi, Mohamed Babu. Viongozi hao walifika kituoni hapo saa 3:00 na kutoka saa 9:00 alasiri. Mwenyekiti Maganja, aliwaambia waandishi wa habari baada ya kuhojiwa kuwa lengo la mahojino hayo ni kupata ukweli wa taarifa za takwimu zilizotolewa kwenye kikao cha kamati kuu ya chama hicho. “Kamati kuu ya chama chetu imeitwa kuhojiwa lakini unajiuliza kuwa polisi wanaweza kuiita Kamati Kuu ya CCM kuwahoji? ili ni jambo la kushangaza sana ndani ya nchi yetu,” alisema Maganja. Alisema wakiwa katika mahojiano hayo walitakiwa kutoa majina ya wajumbe wengine wa kamati hiyo pamoja na namba zao za simu ili waweze kuitwa kuhojiwa, jambo ambalo wamelitekeleza. “Tumewapa namba za simu pamoja na kuwaandikia majina ya wajumbe wengine wa kamati kuu ili waweze kuwaita na kuwahoji kwa sababu wanatoka mikoa tofauti,” alisema.
3
SIMBA inatarajia kutumia jezi za rangi ya kijivu kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Crescentius Magori alisema wamelazimika kutangaza rangi ya jezi hiyo mpya kutimiza matakwa waliyopewa na Shirikisho la Soka Afrika, CAF, kuwataka kuwa na jezi za aina tofauti baada ya kufika hatua ya robo fainali kwenye ligi hiyo msimu uliopita.Simba huvaa jezi nyekundu kwenye mechi za nyumbani na nyeupe kwenye mechi za ugenini, hilo limekuwa kwa muda mrefu kwa michuano mbalimbali. “Ilizoeleka Simba walikuwa na jezi aina mbili, rangi nyekundu na nyeupe ambazo zilikuwa zinavaliwa nyumbani na ugenini. Kwa muktadha huo timu ya Simba kwa sasa itakuwa na jezi aina ya tatu tukiongeza na jezi rangi ya kijivu na hili tumetimiza taratibu tulizopewa na CAF, kutaka kila timu iliyofika hatua hiyo kuwa na jezi ‘nyutro’ ambayo itavaliwa kwenye michuano hiyo kwa msimu unaokuja,” alisema Magori.Katika hatua nyingine, Magori alisema wamempeleka mwanachama wa timu hiyo Hamisi Kilomoni kwenye kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Soka nchini, TFF, ili wamchukulie hatua za kinidhamu kutokana na kuendelea kujitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa yeye ni mdhamini wa klabu hiyo ilihali anajua si kweli.“Sisi kama uongozi wa Simba tumeazimia kumpeleka kwenye kamati ya nidhamu ya TFF ashughulikiwe ili sisi tuende kutolea ushahidi na haki itendeke kwa sababu Simba kampuni hatuna kamati ya nidhamu kama tukiunda itaonekana tumefanya hivi kwa lengo la kumkomoa yeye,” alisema.Alisema Kilomoni alishatolewa kwenye udhamini kwa muda mrefu na sasa inafahamika wazi wanaoshika nafasi hiyo ni Abdu Abbas, Ramesh Patel, Profesa Juma Kapuya na Adam Mgoyi ambao wanafahamika kwa mujibu wa taratibu za kisheria za nchi. Aidha, Magori amebainisha kwamba wiki ya Simba day moja ya mambo watakayoyafanya ni kwenda kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa uwanja wa Bunju.
4
['Manchester United walizomewa na mashabiki wao baada ya Burnley kuweka ushindi wa kwanza katika uwanja wa mechi ya ligi ya Uingereza katika uwanja wa Old Trafford jana Jumtano usiku.', 'Burnley walichukua uongozi kabla ya kipindi cha kwanza baada ya Chris Wood kufunga akiwa maguu sita. ', 'Jay Rodriguez aliongeza bao la pili na kuwapatia The Clarets fursa wakati aliposhirkikana na Wood katika nipe nikupe kabla ya kupiga kombora kali kutoka kona ya upande wa kushoto lililomwacha kipa Davdi de Gea bila jibu. ', 'Ni msimu wa tatu mfululizo kwa Burnley kuwa mbele 2-0 katika uwanja wa Old Trafford, lakini ni mara ya kwanza ambapo walizuia na kutoka na ushindi wa pointi zote tatu. ', 'United waliokosa huduma za mshambuliaji nyota Marcus Rashford , walikuwa na bahati mbaya katika kipindi kirefu na hakuwakuweza kumtishia kipa wa Burnley Nick Pope. ', 'Walisomewa katika kipindi cha mapumziko na baada ya mechi kukamilika na mashabiki wengi walitoka katika uwanja huo katika kipindi cha dakika tano za mwisho. ', "Ole Gunnar Solskjaer's side remain six points behind Chelsea and off the top four, while Burnley climb to 13th, seven points clear of the relegation zone. ", 'Mazungumzo mengi yalikuwa jinsi Man United itakavyocheza bila Rashford ambaye anauguza jeraha kwa kipindi cha wiki sita. ', 'Hiyo ilimpatia fursa Anthony martial kuonyesha umahiri wake kama mshambuliaji wa nyota wa United, akini mshambuliaji huyo alishindwa kufurukuta katika kipindi chote na alikosa nafasi nzuri katika kipindi cha kwanza kupitia pasi za Wan -Bissaka na Nemaja Matic. ', 'Solskjaer alimuingiza kinda mason Greenwood katika kipindi cha kwanza na kijana huyo alionyesha umahiri wake baada ya kumchenga Charlie Taylor na kupiga nje. Hatahivyo hmatokoe hayo ynaweza kuishinikiza United kununua wachezaji wapya katika dirisha dogo la uhamisho la mwezi Januari.', 'Kuna mawazo chungu nzima yanayoendelea akilini mwangu. Wakati mmoja nilifikiria kwamba tunatengeza fursa lakini hatuzitumii. Nimekerwa sana. ', 'Tunakubali kwamba hatukucheza vizuri. Wachezaji wamejitolea, wamefanya kazi nzuri kufikia sasa msimu huu lakini wanajua kwaba hawakuonyesha mchezo mzuri zaidi kutoka na ushindi usiku huu. ', 'Vijana walionekana kuchoka kiakili kufikia mwisho wa mechi, hatakuwa na ubunifu wowote. Hatuwezi kujisamehe. Unapoichezea Man United ni fadhila kwa kuwa unaichezea klabu bora duniani. ', 'Mara nyengine unapitia kipindi kama hiki , najua ni jaribio na nina hakika watakashinda mechi ijayo.', 'Mkufunzi wa Burnley Sean Dyche anasemaje?', ' "Nimefurahia matokeo. Tunajua ni uwanja mgumu kutoka na matokeo na ulikuwa mchezo mzuri. Tulifunga magoli mawili mazuri sana. Hawakuweza kutushambulia, ambacho ni kitu kizuri sana.', 'Manchester United itasafiri kukabiliana na mshindi wa kombe la FA siku ya Alhamisi kati ya Tranmere na Watford siku ya Jumapili tarehe, 26 huku Burnley ikiikaribisha nyumbani Norwich siku ya Jumamosi tarehe 25 Januari.']
4
MEYA mpya wa Jiji la Kigali, Pudence Rubingisa ameahidi kuligeukia jiji hilo kuwa la kibiashara, kwa kuwezesha biashara zote kufanyika katika saa zote za siku, yaani saa 24. Akizungumza hivi karibuni, alisema mbali ya kuimarisha ulinzi katika jiji kwa lengo la kuhakikisha usalama wa raia na mali zao, mikakati inasukwa ya kuhakikisha usafiri unakuwa wa uhakika muda wote. “Lengo ni kutanua wigo wa biashara, ajira kwa wananchi, utoaji huduma za uhakika bila ukomo na juu ya yote, haya yakifanikiwa matokeo yake yataonekana katika ukuaji na maendelo ya kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja, kampuni au mashirika na taifa kwa ujumla,”alisema. Aliongeza kuwa, wanafanyia kazi suala la usafiri wa uhakika kwa kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji. Alisema ndani ya miaka minne, wamelenga kujenga barabara za kisasa za urefu wa kilometa 180 ndani ya jiji huku idadi ya mabasi ikitarajiwa kuongezeka ili yaweze kufanya kasi kwa saa 24. Mipango ya meya huyo inaungwa mkono na Shirikisho la Sekta Binafsi Rwanda (PSF), ikisema itatoa ushirikiano kwa ajili ya ustawi wa shughuli za kiuchumi katika Jiji la Rwanda ambazo zimekuwa zikiimarika mwaka hadi mwaka. Alitoa mfano kuwa katika miaka ya 2000, ilikuwa nadra kuona shughuli au mabasi baada ya saa 2:00 usiku, lakini sasa mabasi yanasafirisha abiria hadi saa 5:00 usiku huku maduka yakiwa wazi hadi saa 4:00 usiku. Theoneste Ntagengerwa, Msemaji wa PSF amesema; “Haya ndiyo mambo tunayoyataka. Tufanye kazi kwa saa 24, naamini wengi wanapata shughuli za kujiingizia kipato,” alisema na kutolea mfano wa kitongoji cha Nyamirambo kuwa wafanyabiashara wengi wa vyakula, vinywaji.
3
Khamis Sharif -Zanzibar  MAKARANI wa uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura katika wametakiwa kufuata kanuni, sheria na miongozo ya uchaguzi ili kutoa huduma bora wakati uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapigakura katika majimbo mbalimbali ya mikoa ya Unguja. Akifungua mafunzo ya siku moja kwa makarani hao mjini Unguja, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Thabit Idarous Faina, alisema matarajio ya tume ni kuandikisha idadi kubwa ya wananchi waliokosa fursa hiyo awali hivyo ni vyema makarani wakawa makini pale wanapotekeleza majukumu yao. Alisema kwa kuwa tume inadhamira ya kuandikisha kila mwenye sifa atakayefika kituoni ni vyema makarani hao wakanyakazi kwa bidi ili kufikia dhamira hiyo ili Wazanzibari waliwengi washiriki katika hatua zote za mchakato wa uchaguzi. Faina alisema tume imekamilisha kazi ya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapiga kwa mikoa yote ya Pemba. Alisema kukamilika kwa kazi ya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapiga kura ni hatua muhimu ambayo itaiwezesha tume kuweka wazi daftari, kugawa vitambulisho vya kupigia kura na kukamilisha kazi ya Uchaguzi Mkuu 2020. Akiwasilisha mada juu ya utaratibu na miongozo ya kazi ya uandikishaji, Mkuu wa Kurugenzi ya Mifumo ya Uchaguzi  wa ZEC, Mwanakombo Machano Abuu, alisema kazi ya uandikishaji itafanyika kwa siku mbili kwa kila kituo cha uandikishaji na kuwataka kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika zoezi la awali. Baadhi ya makarani wa uandikishaji waliahidi kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi sambamba na kuwataka wananchi wenye sifa za kuwemo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kutodharau fursa hiyo ambayo itawapa haki ya kushiriki katika Uchaguzi Mkuu 2020.
3
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam juzi na Naibu Gavana wa BoT, Juma Reli wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya PBZ na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, wateja pamoja na waumini wa dini mbalimbali.Alisema Benki Kuu ndiyo yenye jukumu la kusimamia mifumo ya uendeshaji wa kibenki kwa benki zote zilizopo nchini na kwamba katika kuhakikisha benki za Kiislamu zinafanya kazi zake kulingana na misingi iliyojiwekea ni vyema utaratibu huo ukawepo.“Inatambuliwa wazi kuwa benki hizi zina utaratibu wa utoaji wa huduma kwa kuzingatia masuala ya riba, BoT imeona vyema kuwa na kanuni maalumu zitazoziwezesha benki hizo kufanya kazi zake kwa utaratibu unaoeleweka ili kuziondolea usumbufu,” alisema.Alisema katika kuhakikisha hilo linatekelezeka tayari mchakato wa uandaaji wa kanuni hizo umeshaanza kufanyiwa kazi na wakati wowote utakapokuwa umekamilika utaingizwa katika utaratibu kwa ajili ya utekelezaji.Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya PBZ mmoja wa viongozi wa benki hiyo Said Said alisema benki hiyo yenye idadi ya matawi manne Tanzania Bara na Zanzibar inazidi kujiimarisha kadri siku zinavyokwenda na hivyo kuwapa imani ya kuwa na nguvu zaidi miaka ijayo.
5
MOSCOW, URUSI NDEGE ya Jeshi la Urusi iliyokuwa na watu 92 wakiwamo waimbaji, wanenguaji na wanamuziki wengine wa Jeshi la Urusi ilianguka katika Bahari Nyeusi wakati ikielekea Syria jana na kuwaua watu wote hao. Kwa mujibu wa maofisa wa Urusi, wanamuziki hao walitarajia kufanya tamasha ya mwaka mpya katika kambi ya Urusi mjini Latakia, Syria. Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi, ndege hiyo aina ya TU-154 Tupolev ilitoweka kutoka rada alfajiri ya jana, dakika mbili tu baada ya kuruka kutoka Sochi, kusini mwa Urusi, ambako ilisimama kwa muda kujaza mafuta ikitokea Moscow njiani kuelekea Syria. Msemaji wa wizara hiyo, Meja Jenerali Igor Konashenkov, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hakuna aliyenusurika katika ajali hiyo. Eneo la ajali limeshabainishwa na tayari meli, helikopta na ndege zisizotumia na rubani zimeanzisha uchunguzi huku mabaki yakiripotiwa kupatikana kilomita moja na nusu kutoka pwani. Aidha chanzo kimoja cha habari kilisema ndege hiyo haikuwa imetuma tahadhari na hapakuwa na ishara ya kuwepo matatizo, na rubani alikuwa ametulia hadi ndege hiyo inatoweka. Katika taarifa yake kwa njia ya televisheni, akiwa mji wake wa nyumbani wa St. Petersburg, Rais wa Urusi Vladimir Putin ametangaza leo kuwa ni siku ya kitaifa ya maombolezo. Ndege hiyo iliyotengenezwa mwaka 1983 wakati wa zama za Muungano wa Kisovieti, ilikuwa imebeba abiria 84 na wafanyakazi wanane.
2
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka wanawake wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, kuzitumia huduma za mama na watoto katika hospitali hiyo yenye huduma zote, ikiwemo za uzazi salama.Samia alisema hayo wakati akiweka jiwe la msingi jengo la kutoa huduma za kujifungua kwa wanawake katika Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja. Alisema juhudi za kupunguza vifo vinavyotokana na wanawake kujifungua, vitapungua tu kama wanawake hao watapata huduma hizo katika vituo vya afya vya Serikali.Alisema bado wapo wanawake nchini, wanajifungua majumbani bila ya huduma za madaktari wenye uwezo na kutishia vifo kwa watoto. “Wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguj, serikali imeimarisha huduma za wanawake na watoto, kwa hiyo mnatakiwa kujifungua katika hospitali za serikali na kupata huduma kutoka kwa madaktari bingwa,” alisema.Mapema, Katibu Mkuu, Wizara ya Afya Asha Ali Abdalla alisema serikali imeongeza bajeti wizara hiyo kutoka Sh 7,000,000,000 katika mwaka 2018 hadi Sh bilioni 15 katika mwaka wa fedha 2019-2020.“Sekta ya afya imepewa kipaumbele cha kwanza na hata bajeti ya Wizara ya Fedha imekuwa ikiongeza siku hadi siku kwa maslahi ya wananchi wake,” alisema.Mapema, Waziri wa Afya, Hamad Rashid Mohamed alisema huduma za matibabu Zanzibar, zitaendelea kutolewa bure kwa wananchi wote, ikiwa ni kutekeleza ahadi ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume. Alisema huduma za afya zinaendelea kuboreshwa, ikiwemo za wanawake wajawazito kwa ajili ya kupunguza vifo vya watoto vinavyotokana na matatizo ya uzazi.“Tutaendelea kutoa huduma za fya bure huku kipaumbele chetu ni kwa wanawake kujifungua katika hospitali za serikali na kupata huduma hizo bure zikiwa za uhakika,” alisema.
3
WAZIRI wa Nishati, Dk Medard Kalemani ameagiza kusimamishwa kazi maofisa wawili wa juu wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), ili kupisha uchunguzi baada ya nchi kukumbwa na katikakatika umeme ndani ya miezi miwili.Dk Kalemani alitoa maelekezo hayo juzi jioni jijini hapa baada ya kukutana na viongozi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Tanesco. Alitoa siku saba kuanzia Jumamosi kwa bodi hiyo kuunda tume itakayochunguza suala hilo.“Bodi lazima ichukue hatua kuhakikisha kinachosemwa gridi kutoka, gridi haitoki na kusababisha nchi nzima au sehemu ya nchi kukosa umeme. Lazima mchukue hatua za makusudi kuhakikisha hilo halijitokezi tena.“Maelekezo yangu kwa menejimenti kupitia Mwenyekiti wa Bodi, unda timu mahususi kuanzia leo (juzi) ya kuchunguza na kufuatilia jambo hili kwa kuhusisha tasnia na taasisi mbalimbali sio Tanesco peke yake. Ndani ya siku saba nipate matokeo ya nini chanzo cha tatizo hilo ili lisijirudie kabisa,” aliagiza Waziri.“Jambo linapotokea ina maana kuna uzembe katika usimamizi, au kutofuatilia maelekezo ya serikali, au kunaweza kuwa na hujuma kwa baadhi ya watumishi wasiokuwa wazalendo.“Kwa hiyo kuanzia leo (juzi), Bodi ichukue hatua mahususi za kiutawala dhidi ya Naibu Mkurugenzi wa generation na Naibu Mkurugenzi wa transmission, ikiwa ni pamoja na kuwavua nyadhifa zao,” alisema.“Haya yanatokana na uzembe au kutochukua hatua au kutowawajibisha watu wa chini yao, jambo hili limejitokeza mara nyingi. Haiwezekani nchi ibaki kwenye giza nusu saa, maana yake usalama wa nchi haupo, haiwezekani viwanda visimame ndani ya nusu saa maana yake uzalishaji unasimama na kodi ya serikali inapotea, hawa watu waanze kuchunguzwa mara moja na wote wanaohusika,” alisisitiza Waziri Kalemani.Dk Kalemani alisema ametaarifiwa kuwa nchi ilikabiliwa na tatizo la kukatikatika umeme kati ya Novemba 28 na 30 na Desemba 4 na 14 kutokana na kutokea hitilafu gridi ya taifa na kusisitiza hiyo ni hatari kwa usalama wa nchi. Alisema maofisa hao wa juu wa Tanesco wanapaswa kueleza ni kwa nini nchi imepatwa na tatizo la kukatikakatika umeme mara nne ndani ya miezi mwili wakati nchi inazalisha ziada ya umeme megawati 252 gridi ya Taifa.Waziri aliagiza bodi hiyo kuhakikisha maeneo ya mijini ambayo hayajaunganishiwa huduma ya umeme na yanasubiri kuunganishwa yapelekewe ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa.“Yako maeneo ya mijini ambayo hayahitaji kuunganishwa umeme na yamekaa bila kuunganishiwa muda mrefu huku yako ndani ya mipango ya shirika na fedha imeshatoka kila mkoa. Tunataka kuona ndani ya miezi mitatu wamefikishiwa huduma hiyo.Na hii ni kazi yako mwenyekiti wa bodi, toa maelekezo kwenye menejimenti yako,” aliagiza Waziri. Pia aliiagiza Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco kuhakikisha ifikapo Desemba 30, mwaka huu, iwe imewaunganishia umeme wateja wote nchi nzima ambao wameshalipia gharama za kuunganisha umeme na hawajapewa huduma.“Kuna wateja ambao wameshalipia gharama za kuunganishiwa umeme, miezi miwili, mmoja, mitatu na hawajaunganishwa. Naagiza wateja wa aina hii nchi nzima wawe wameunganishiwa umeme hadi Desemba 30 mwaka huu,” alisema.
3
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Januari Makamba amesema Watanzania wengi watapata kipato kwa kutengeneza, kuuza na kusambaza mifuko mbadala baada ya zuio la matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia Juni mosi, mwaka huu.Alisema mbali ya kipato hatua hiyo pia itawezesha wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani ya nchi kuanzisha viwanda vidogo vya kutengeneza mifuko mbadala, hatua itakayokuza uchumi na kuzalisha ajira.Aliyasema hayo juzi alipokutana na kufanya mazungumzo na watendaji wa taasisi mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam. Alisema zaidi ya nchi 60 tayari zimepiga marufuku matumizi ya mifuko ya aina hiyo na maisha yanakwenda vizuri bila uharibifu wa mazingira.Aliwataka Watanzania wawe na mtazamo chanya wa zuio hilo na kusema kwamba ilipita miaka 30 baada ya Uhuru mifuko ya plastiki kuanza kutumika nchini na maisha yalikwenda vizuri.Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mwita Waitara alisema serikali imejipanga kusimamia marufuku hiyo ya matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia ngazi ya mtaa hadi mkoa.Alisema pia maandalizi yamefanywa kupeleka elimu juu ya jambo hilo kupitia shule za msingi, sekondari na kwenye mikusanyiko ya ibada. “Kila liliko kusanyiko la ibada tutawaomba viongozi tutoe elimu juu ya zuio hili ili wananchi washirikiane na serikali,” alisema.Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dk Samuel Gwamaka, alisema baraza litatumia kanda zake saba kuhakikisha utekelezaji wa zuio hilo unakwenda vizuri kwa kushirikiana na mikoa kuandaa maeneo ya kuhifadhi masalia ya mifuko baada ya zuio.
3
LYON, ITALIA KLABU  ya  Lyon imejiondoa katika mipango  ya  kumsajili aliyekuwa mshambuliaji wa  timu ya  Arsenal, Manchester City na Tottenham,  Emmanuel Adebayor (32). Adebayor ambaye ni mchezaji huru  baada ya kumaliza  mkataba  wake  na klabu ya  Crystal Palace, alikuwa mbioni kujiunga na timu ya  Lyon. Nyota huyo wa Togo, Ijumaa iliyopita alikuwa jijini Lyon, Ufaransa kwa ajili ya mazungumzo na  kocha wa Lyon, Bruno Genesio. Lakini klabu hiyo  haikukubaliana na nyota huyo  kutokana na umri wake kuwa mkubwa,  huku ikidai kwamba   atashindwa kuwa na msaada katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambayo timu hiyo inashiriki msimu huu. Klabu hiyo  inayoshiriki Ligi Kuu  ya Ufaransa  (Ligue 1), pia ilidai  haitafurahishwa  na hatua za kumkosa mchezaji huyo kwa miezi miwili ya msimu huu  wakati  akiwa na  timu yake ya taifa  katika Kombe la Mataifa  barani Afrika. Katika hatua nyingine, Lyon ilisema ina furaha kumsajili mshambuliaji mwengine,  Jean Phillipe Mateta, baada ya Adebayor kusema kuwa angependa kuliwakilisha taifa lake katika kombe la bara Afrika mapema 2017, hatua ambayo ingemfanya kutochezea timu hiyo kati ya mwezi mmoja hadi miwili.
4
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ilimlazimu kufi ka hadi saa mbili na nusu usiku wakati akishughulikia migogoro ya ardhi katika wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.Hali hiyo ilitokana na wananchi kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Kampala uliopo Gongo la Mboto, ikiwa ni siku yake ya kwanza ya ziara ya kushughulikia migogoro ya ardhi katika wilaya zote za jiji la Dar es Salaam kupitia program ya Funguka kwa Waziri.Wakati akianza mkutano wa kushughulikia migogoro ya ardhi katika wilaya ya Ilala ilielezwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Sophia Mjema kuwa, takribani wananchi 241 walijiandikisha kwa ajili ya kutatuliwa kero zao za ardhi, lakini kadri muda ulivyokuwa ukiongezeka idadi iliongezeka na kufikia zaidi ya 400.Kutokana na hali hiyo, Waziri Lukuvi aliamua kuendelea kuhudumia wananchi wote waliojitokeza hadi saa 2.30 usiku, jambo lilolazimu taa za magari likiwamo la waziri huyo kutumika kwa ajili ya kupata mwanga na hivyo kukamilisha utaratibu huo.Uamuzi wa kuendelea na mkutano hadi usiku uliwafanya baadhi ya wananchi kumuelezea Waziri Lukuvi kama kiongozi anayeshughulika na matatizo ya wananchi katika maeneo husika bila kujali muda.Mmoja wa wakazi wa Gongo la Mboto, James Jonathan alimuelezea Lukuvi kama Waziri aliyeimudu vyema Wizara ya Ardhi kutokana na jinsi anavyohangaika maeneo mbalimbali ya nchi kwa nia ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imekuwa kero kubwa kwa wananchi.Mkazi mwingine, Athumani Juma Mrisho alisema programu ya Funguka kwa Waziri inayotumika sasa imekuwa suluhisho la migogoro ya ardhi nchini ambapo wananchi wanapata fursa ya kuwasilisha malalamiko yao moja kwa moja kwa waziri mwenye dhamana ya ardhi, jambo ambalo huko nyuma wananchi hawakuwa na fursa hiyo na hivyo kusababisha malalamiko mengi kutomfikia waziri.Akihitimisha mkutano wake na wananchi wa wilaya ya Ilala, Waziri Lukuvi aliwataka watendaji wa sekta ya ardhi kuhakikisha hoja zote za migogoro ya ardhi zilizowasilishwa kwake zinainishwa na kupatiwa majibu ya maandishi kama alivyoelekeza. Aidha, alisisitiza kuwa ifikapo Februari 28, mwaka huu, majibu hayo yawe yamekamilika na kuwekwa katika kitabu maalumu kitakachokuwa na nakala tatu zitakazosambazwa kwake, Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya.Alisema, uamuzi wa kufanya hivyo ni kuweka kumbukumbu sawa ili hata akija kiongozi mwingine aweze kufahamu matatizo yaliyopo tofauti na ilivyokuwa sasa ambapo hoja za migogoro ya ardhi zimekuwa zikijirudia hasa yanapotokea mabadiliko ya viongozi katika ngazi mbalimbali. Alifafanua kuwa kwa yule mwananchi asiyeridhika na majibu yatakayotolewa, basi awasilishe tatizo lake kwa njia ya maandishi kwa Waziri.
3
SERIKALI kwa kushirikiana na serikali ya Canada imetumia dola milioni 53 sawa na Sh bilioni 92 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ubora wa elimu kwa ualimu (TESP) ambapo ni miundombinu, mfumo wa Tehama na vitendea kazi katika vyuo vya ualimu 35 nchi nzima.Mratibu wa mradi huo wa Tesp kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolijia Ignas Chonya amesema, kompyuta 780 tayari zimesambazwa vyuo vyote, UPS 780, projekta 100, mashine kwa ajili ya kutoa kopi na kuchapisha nyaraka mbali mbali.“Kwa sasa tunamalizia kuunganisha vyuo vyote katika mkongo wa taifa na kuanza kutumika kubadilishana mfumo wa ufundishaji ,” amesema ChonyaAmesema kuunganishwa kwa vyuo katika mkongo wa taifa kutasaidia walimu kuwasiliana na kuendesha mafunzo kwa mfumo wa mtandao (E- Learning).“Tumeona madaktari wanafanya upasuaji kwa njia ya mtandao kwa kushirikiana na wenzao waliopo nje au mkoa mwingine, sasa tunataka na walimu wafikie teknolojia hiyo,” alisema.Vyuo vilivyonufaika na msaada huo ni Dakawa, Ilonga, Mandaka, Mhonda, Mrutunguru, Mamire, Ndala, Singachini, Shinyanga na Kabonga Vyuo vingine ni Patandi, Tarime, Mpuguso, Sumbawanga, Mpwapwa, Tukuyu, Morogoro na KorogweAlisema mpaka mwezi Oktoba mwaka huu, vyuo vyote hivyo vitakuwa tayari vimeshaunganishwa kwenye kanzi data na kuanza kufanya kazi.Chonya alisema mpaka sasa wakufunzi 731 wameshapatiwa mafunzo hayo ya Tehama ambapo serikali inaamini hiyo itakuwa chachu katika mapinduzi ya elimu nchini, kwani wanafunzi wataanza kufundishwa teknolojia hiyo ya habari (Tehama) kwa vitendo tangu elimu ya awali.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa leo kufungua kongamano la biashara na uwekezaji la Mkoa wa Pwani ambalo Wizara ya Nishati imesema itaeleza mwelekeo wa sekta ya nishati katika kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji katika viwanda. Aidha, katika kongamano hilo linalofanyika sanjari na maonesho ya viwanda mjini Kibaha, Waziri Mkuu anazindua mwongozo wa uwekezaji unaoanisha fursa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa wa Pwani.Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo alitoa taarifa hiyo juzi kwenye ufunguzi wa maonesho ya viwanda ambayo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan aliyewakilishwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Stella Manyanya.“Maonesho ya mwaka huu yataambatana na kongamano la uwekezaji na kongamano hili litafanyika keshokutwa (leo) ambapo mwongozo wa uwekezaji wa mkoa wa Pwani utazinduliwa na Waziri Mkuu,” alisema Ndikilo.Akizungumza hivi karibuni juu ya mwongozo wa uwekezaji, Ndikilo alisema umetayarishwa na Taasisi ya Uafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) ofisi ya Tanzania. Mwongozo umeainisha fursa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa wa Pwani kwenye sekta ya kilimo, uvuvi, utalii, ujenzi wa viwanda na huduma za jamii. Mkuu wa mkoa alisema wamejiridhisha yaliyomo katika mwongozo huo ndiyo picha halisi ya mkoa wa Pwani.“Mtu atakayebahatika kufunua mwongozo huu basi atatuona vizuri ni nini tulicho nacho katika mkoa wetu wa Pwani,” alisema. Naibu wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza kwenye ufunguzi wa maonesho ya viwanda juzi, alisema wakati wa kongamano wizara yake itaelezea mwelekeo wa sekta ya nishati katika kuweka mazingira wezeshi ya viwanda. Alitoa mfano wa umeme kukatika mara kwa mara na kusema serikali inafanya kila linalowezekana kuhakikisha kunakuwa na umeme wa uhakika na kuongeza kuwa mahitaji ya umeme mkoa wa Pwani yameongezeka kwa kufika megawati 82. Alisema kutokana na wawekezaji wengi kuwa maeneo ya wilayani, serikali inatekeleza mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vijiji 150 mkoani Pwani. “Tuna sekta ya gesi asilia. Tunataka tuwahakikishie wenye viwanda, tunataka tuawaandalie mazingira ya kupunguza gharama za uzalishaji,” alisema na kuongeza kuwa gesi ipo ya kutosha na miundombinu hususani bomba la gesi la taifa linalotoka Mtwara hadi Dar es Salaam.Naibu Waziri huyo alisema serikali imesikia pia kilio cha wenye viwanda juu ya bei kubwa ya gesi na kuongeza kuwa Waziri wa Nishati, Medard Kalemani alitoa mwezi kwa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) kukaa na wadau mbalimbali kusikiliza maoni yao ili waje na bei itakayosaidia wawekezaji kupunguza gharama za uzalishaji kama yalivyo maelekezo ya Rais John Magufuli. Hivi karibuni, timu ya waandishi wa habari kutoka kampuni ya magazeti ya serikali, Tanzania Standard Newspapers (TSN) iliyotembelea viwanda mbalimbali mkoani Pwani, ilielezwa namna umeme usioaminika unavyowasababishia hasara.Kongamano la biashara na uwekezaji linakwenda sanjari na maonesho ya wazi ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na viwanda vidogo, kati na vikubwa yanaendelea katika viunga vya ofisi ya mkuu wa mkoa mjini Kibaha.
3
Mkutano huo utakaofanyika Bagamoyo, unalenga kujadili ni namna gani nchi za Afrika zitaondokana na kuuza nje bidhaa ghafi ambazo zinazipatia nchi hizo fedha kidogo za kigeni.Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kukuza na Kuchochea Ushindani wa Maendeleo Barani Afrika (PACF) Profesa Burton Mwamila, alisema mkutano huo umeandaliwa na jumuiya ambayo ilianzishwa kwa msaada wa Umoja wa Afrika (AU) pamoja na Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida).Profesa Mwamila alisema washiriki kutoka nchi 10 za Afrika watahudhuria mkutano huo ambao umeanza jana jioni huku kongano bunifu zipatazo 40 za Watanzania zitahudhuria mkutano huo.Wazalishaji hao watapata fursa ya kuonesha bidhaa mbalimbali ambazo wamezibuni ambazo baadhi yake zinauzwa nje ya nchi.Tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo inayohusisha Serikali, wanataaluma na wazalishaji, Tanzania kumeanzishwa kongano bunifu 70, jambo ambalo Profesa Mwamila analielezea kuwa ni mafanikio makubwa yenye lengo la kuiletea nchi maendeleo.Alisema sekta ndogo za viwanda, wajasiriamali kwa kuwatumia wasomi na wabunifu ndio wenye fursa kubwa ya kuleta maendeleo kwa taifa kama zilivyofanikiwa nchi za Magharibi ambazo sekta hiyo ndiyo ya viwanda ndiyo inaajiri watu wengi zaidi kuliko sekta kubwa.Alisema wakati wa mkutano huo, wabunifu na wazalishaji watapata ujuzi wa kuboresha bidhaa zao na kuziuza nje vikiwemo vikundi vya wabunifu ambavyo vinadhaminiwa na Shirika la Kuendeleza Viwanda Vidogo nchini (Sido).Naye kiongozi wa jumuiya hiyo nchini, Sosthenes Sambua alisema lengo la jumuiya yake kuandaa mikutano hii ni kutaka Watanzania kutumia ubunifu wa rasilimali zilizopo nchini waweze kuongeza thamani ya bidhaa zao na kuziuza nje kwa fedha kubwa kuliko wakiuza kwenye malighafi.Alisema Serikali pekee haiwezi kuwaletea wananchi wake maendeleo bila kutumia wanataaluma waliopo nchini. Mkurugenzi wa Sido, Omari Bakari alisema jumuiya hiyo imekuwa chachu kubwa kwa vikundi vinavyodhamiwa na taasisi yake katika kubuni viwanda vidogo ambavyo vinawaletea wananchi maendeleo.
5
Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam HOSPITALI ya Taifa ya Afya ya Akili, Mirembe, imefanya mabadiliko katika utoaji wa huduma za matibabu kwa wagonjwa wa nje, ambapo muda wa kuanza kutoa matibabu ni saa moja asubuhi badala ya saa mbili asubuhi. Lengo la uongozi wa hospitali kufanya mabadiliko hayo ni kuboresha huduma za afya ili kuwezesha watu mbalimbali kupata huduma za matibabu mapema zaidi na kwa wakati. Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe, Dk. Paul Lawala, alisema mabadiliko hayo yanahusu huduma zote za afya, ikiwamo huduma za afya ya akili pamoja na magonjwa ya mwili. Dk. Lawala alisema tangu kuanza kwa utekelezaji wa mabadiliko hayo,  kumekuwapo na matokeo chanya kwa kuwa watumishi wamefurahia kuanza kutoa huduma mapema, huku wagonjwa na ndugu wakifurahia utaratibu mpya wa kupatiwa huduma mapema na kurejea nyumbani mapema. “Matokeo chanya yameanza kuonekana kwani watumishi wameitikia wito wa kuwahi mapema na kuanza kutoa huduma saa moja asubuhi. “Hatua hii imesaidia watu kupata huduma za matibabu mapema na kwa wakati na pia watu wengi wamevutiwa na mabadiliko haya,” alisema Dk. Lawala. Naye Mkuu wa Kitengo Cha Wagonjwa wa Nje, Dk. Isack Mrimi, aliwataka wananchi kufika katika  hospitali hiyo kupata huduma za matibabu kwa kuwa Mirembe ina wataalamu wabobezi wenye uwezo wa kutoa huduma bora na kwa wakati.
3
UGONJWA wa shinikizo la damu (BP) umeonekana kuwa tatizo mkoani Mtwara kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya wagonjwa kati ya 50 hadi 60 kwa siku.Idadi hiyo imebainika wakati jopo la madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), walipotoa huduma za kitabibu katika Hospitali ya Rufaa ya Ligula mkoani hapa.Madaktari hao wameeleza kushitushwa baada ya kuona idadi hiyo kubwa ya wagonjwa hao mkoani humo.Wameomba kufanyika kwa kazi maalum ya utafiti wa haraka ili kujua chanzo na sababu inayosababisha kushamiri kwa maradhi hayo kwenye jamii.Kazi hiyo ilifanyika ndani ya wiki moja mkoani hapa, huku Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi, Geofrey Marandu akitoa tathimini ya utendaji kazi ndani ya siku hizo kuwa katika Hospitali hiyo ya Ligula, wamekuwa wakihudumia idadi hiyo kubwa ya wagonjwa kwa siku hali ambayo si ya kawaida."Tumeshitushwa sana na idadi kubwa ya wagonjwa wa shinikizo la damu mkoani hapa kwa kweli hii si idadi ya kawaida na natoe wito wa kufanyika utafiti wa haraka kujua sababu ya kukithiri kwa maradhi haya wagonjwa 50 hadi 60 kwa siku si idadi ya kawaida."Tumebaini uwepo wa wagonjwa wengi wa shinikizo la damu kwa siku zote hizo na tumekuwa tukipokea wangonjwa kati ya 50 hadi 60. Utamkuta mgonjwa ana BP 220/120 lakini mwenyewe haoni kama ana tatizo na wala hajali yuko kawaida tu" amesema.Amesema kuwa kunahitajika kufanyika kwa utafiti wa kina ili kubaini tatizo hilo, ambalo watu wengi wa Mtwara wamekuwa nalo, kwani maradhi hayo yana uhusiano mkubwa na maradhi ya moyo, damu na mengine.Mbali na tatizo hilo, amesema pia wagonjwa wa macho na uvimbe tumboni kwa wanawake walihudumiwa kwa wingi, ukilinganisha na magonjwa mengine.Pia, amesema magonjwa ya macho yameonekana kuwa tatizo kubwa, kwani yamebainika kuwa ni ugonjwa mbaya na huwaathiri watu wengi na matibabu yake yakicheleweshwa husababisha upofu.Amesema, katika kipindi hicho, wameweza kuwahudumia wagonjwa 1,467 huku lengo likiwa kuwafikia wagonjwa 2,000 na kati yao 54 walifanyiwa upasuaji mkubwa na 81 upasuaji mdogo.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Dk Lobikieki Kissambu amesema kazi hiyo imeonesha mafanikio makubwa, licha ya changamoto ya baadhi ya wagonjwa kutokamilisha matibabu kutokana na kushindwa kuchangia gharama."Zoezi hili halikuwa bure, mgonjwa alilazimika kuchangia fedha kidogo, wapo wagonjwa walioandikiwa upasuaji lakini muda ulipofika hawakuonekana kwa sababu walishindwa kulipia gharama licha ya kuwa ndogo," amesema Kissambu.Alitoa rai kwa jamii mkoani hapa kuwa ili kuepukana na hali hiyo ni muhimu wananchi wakajiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kurahisisha matibabu pindi wakosapo fedha.
3
Taarifa iliyotolewa jana na kampuni hiyo, imesema wamefanya hivyo kuhakikisha wakazi wa Mbezi Beach na maeneo jirani ya Tegeta, Kawe na Boko wanapata huduma kwa karibu.Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia alisema kitongoji hicho, ni miongoni mwa maeneo ya jiji yanayokua kwa kasi kwa maendeleo na kivutio cha wawekezaji wengi.Alisema wamezingatia idadi kubwa ya watu na shughuli mbalimbali za kibiashara ikiwemo maofisi, hoteli na pia kuwa njia kuu ya kuelekea katika mji wa kihistoria wa Bagamoyo, Pwani.“Duka hili jipya lenye mazingira rafiki kwa wateja litakuwa linatoa huduma mbalimbali kwa wateja wa Vodacom ikiwemo huduma kwa mawakala wa M-pesa na uuzaji wa bidhaa mbalimbali za Vodacom,” alisema.Mworia alisema ufunguzi wa duka hilo ni mwendelezo wa malengo ya Vodacom kuboresha maisha kwa wananchi kwa kuwapatia huduma zenye ubora na kuwafikia wateja kwa urahisi. Mkazi wa Mbezi Beach na mteja wa kwanza kupata huduma katika duka hilo baada ya kuzinduliwa, Argylle Tsvakai aliipongeza hatua ya kusogezewa huduma karibu.Vodacom ina mtandao wa maduka 87 na wakala mbalimbali wa kuuza bidhaa zake nchini na duka lililofunguliwa jana ni la 88 katika wilaya ya Kinondoni.
5
TANZANIA imeziomba nchi tajiri duniani, kuongeza michango ya kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi walau kufi kia dola za Marekani bilioni 100 kila mwaka.Akihutubia Mkutano wa 25 wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya Tabianchi unaomalizika jijini Madrid nchini Hispania, Naibu Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Musa Sima amesema Tanzania imeathiriwa sana na matukio ya janga la tabianchi, hasa kwa matukio ya mvua nyingi na joto lililopitiliza ambavyo havikupata kushuhudiwa kwa miongo kadhaa iliyopita.Sima alisema mafuriko yameua, yameharibu barabara na madaraja na kusababisha hasara kubwa.Alisema Tazania inatambua machango wa nchi tajiri katika kupambana na janga hilo la kidunia, lakini alikumbusha kwamba nchi tajiri zimeahidi kutoa kwa hiari fedha za ziada kwenye mfuko uitwao Green Climate Fund – ahadi ikiwa ni dola za Marekani bilioni 9.66.Alikumbusha, “bado tuko mbali na kuziba pengo la mahitaji ya fedha ya nchi zinazoendelea na lengo lililowekwa la kukusanya dola za Marekani bilioni 100 kwa mwaka. Kwa hiyo, tunaziomba nchi zilizoendelea na wachangiaji wengine kuzidisha michango yao.”Alisema katika kutoa mchango wake kidunia, Tanzania inatekeleza miradi kadhaa ya kimkakati ili kupambana na athari za tabianchi na kutaja baadhi yake kuwa ni ujenzi wa miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia maji.Aidha, Tanzania imeimarisha Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa (TMA) kwa kununua rada mbili ili kuiongezea uwezo taasisi hiyo wa kufuatilia na kutabiri mwenendo wa hali ya hewa. Ili kupunguza uotoaji wa gesimkaa, Sima alieleza kwamba Tanzania imejenga Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) katika Jiji la Dar es Salaam na inajenga Reli ya Kisasa (SGR).Pia amesema Tanzania iko makini na kampeni ya kitaifa ya kupanda miti ili kupambana na upoteaji na uharibifu wa misitu. Alieleza kwamba Tanzania inaendesha kampeni hiyo, ingawa ina takribani hekta milioni 48 za misitu.Amesema Tanzania inazishukuru serikali za Chile na wenyeji wa mkutano, Hispania kwa kuandaa mkutano huo. Tanzania ilimshukuru Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kwa kuandaa mkutano wa wakuu wa nchi, uliofanyika jijini New York Septemba 23, mwaka huu.Sima amesema kwa ushahidi wa ripoti ya mwaka huu ya taasisi ya IPCC na maonyo yake.Maonyo ya mwaka huu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa (WMO), dunia ina wajibu wa kuchukua hatua za haraka kulinda sayari hii na wakati wa kufanya hivyo ni sasa.
3
WATANZANIA 22 waliozamia nchini Afrika Kusini wamehukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kutumikia kifungo cha miezi sita jela baada ya kukiri kuondoka nchini bila kufuata taratibu.Washitakiwa hao ni Mzuzuri Mohammed, Mohammed Said, Masoro Musa, Mneke Mehra, Kibila Husein, Ali Hassan, Jamalino Rashid, Abdul Nassoro, Waziru Adam na Said Salum.Wengine ni Chuwa Sadick, Salum Kasimum, Macalot Alex, Kayenga Winston, Idali Charles, Ibrahim Mohammed, Jafari Zebra, Omane Fizo, Mbona Edson, Ulembo Azide, Fizo Charles na Mnangwa Rajab.Akitoa adhabu hiyo, Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo alisema anawatia hatiani kwa kuondoka nchini bila kufuata sheria za uhamiaji na kwamba akiwaangalia washitakiwa wote ni vijana wenye nguvu na ambao wangeweza kufanya kazi za kujenga taifa.Alisema wameliingizia gharama taifa kwa kukodi ndege ya kuweza kuwarudisha nchini wakati fedha hizo zingeweza kujengea hospitali na kufanya shughuli nyingine za maendeleo.“Makosa haya yamekuwa yakijirudia hivyo mahakama hii inawapa adhabu ya kifungo cha miezi sita jela na mkafanye kazi mbalimbali mtakazopangiwa na magereza,” alisema Hakimu Mwaikambo.Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo, Wakili wa Serikali, Shija Sitta aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa vijana wengine.Alidai taratibu za kusafiri nje ya nchi zipo na kwamba hakuna msingi wa watu kwenda Afrika Kusini bila kibali kitendo ambacho kimedhalilisha taifa kwa kuonekana ni wahamiaji haramu.Washitakiwa hao kwa nyakati tofauti waliiomba mahakama iwapunguzie adhabu ili kulitumikia taifa.Awali, akisoma mashitaka, Sitta alidai washitakiwa hao walitoka nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinyume na kanuni za uhamiaji namba 20 (3) (a) G.N namba 657 ya mwaka 1997 inayosomwa pamoja na kifungu namba 48 (2) ya Sheria ya Uhamiaji namba 54 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016.
3
NA WINIFRIDA MTOI         |                 PAZIA la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2018/2019, linatarajia kufunguliwa leo huku ikiwa haina mdhamini mkuu baada ya Kampuni ya simu ya Vodacom kumaliza mkataba wake. Mbali na kutokuwa na mdhamini, msimu huu idadi ya timu imeongezeka kutoka 16 hadi 20, hivyo kuna uwezekano mkubwa timu nyingi kushindwa kufika vituoni kutokana na kukosa fedha. Wadhamini waliojitokeza hadi sasa ni Kampuni ya Azam na Benki ya KCB ya Kenya. Ligi hiyo itaanza kwa mechi sita kupigwa leo katika viwanja tofauti lakini kati ya hizo mchezo unaotarajia kuvuta hisia za wapenzi wengi wa soka ni ule unaohusisha mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Simba watakaowakaribisha Tanzania Prisons Uwanja wa Uhuru,  jijini Dar es Salaam. Simba watashuka dimbani wakiwa ni mabingwa wa Ngao ya Jamii kwa mwaka huu wakitwaa kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuifunga Mtibwa Sugar mabao 2-1, katika mechi iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita katika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. Wekundu wa Msimbazi, watavaana na Prisons 1:00 usiku badala ya saa 10:00 kama ilivyopangwa awali kutokana na Sikukuu ya Idd Alhaj. Hamu kubwa ya mashabiki wa kikosi hicho ni kutaka kuona ubora wa timu yao katika mechi za Ligi Kuu kama itaendeleza ubabe baada ya kufanya vizuri kwenye mechi za kirafiki, Simba Day dhidi ya Asante Kotoko ya Ghana na Ngao ya Jamii dhidi ya Mtibwa Sugar. Tofauti na hilo, pia Wanasimba wengi wanahamu ya kuona matunda ya kambi ya timu yao waliyokuwa wameweka nchini Uturuki pamoja na ubora wa wachezaji wapya. Simba iliweka kambi ya wiki mbili Uturuki kwa lengo la kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ambako walifanikiwa kucheza mechi tatu za kirafiki. Ikumbukwe kuwa baada ya kumalizika kwa ligi ya msimu uliopita, Simba walifanya usajili mkubwa kwa kuchukua wachezaji walioonyesha viwango vya juu katika timu mbalimbali, ndani na nje ya Tanzania. Tayari wachezaji; Meddie Kagere,  Cletus Chama, Adam Salamba, wameonekana kuwateka wapenzi wa Simba kutokana na kiwango walichokionyesha katika mechi kadhaa,  lakini bado ubora wao utadhihirika pale watakapoonyesha makali yao kwenye ligi hiyo. Hassani Dilunga naye baada ya kuwakosha mashabiki wa Wekundu hao,  alipofunga bao la ushidi dhidi ya timu yake ya zamani Mtibwa  Sugar katika mechi ya Ngao ya Jamii, wakimsubiri kumwona akifanya vizuri kwenye mchezo wa leo, ni wazi atawaaminisha wadau wa kikosi hicho kuwa hakubahatisha. Katika mechi za hivi karibuni tumeona pacha ya washambuliaji wa Simba, Kagere na Emmanuel Okwi, ikiwa na mafanikio makubwa, je, kwenye ligi itaendelea hivyo? Picha kamili itaanza kuonekana leo. Kwa upande wa Kocha Mkuu Mbelgiji, Patrick Aussems, atakuwa na kibarua kigumu kuhakikisha anapata matokeo mazuri kwa sababu utakuwa ni mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu tangu akabidhiwe kikosi hicho. Ukiangalia kikosi cha Prisons wanachokutana nacho Simba, ni moja ya timu ngumu katika ligi hiyo, hivyo haitakuwa mechi rahisi ya kujiaminisha kupata matokeo mazuri bila kupambana. Katika kudhihirisha hilo, kocha wa Simba, Aussems, baada ya mechi na Mtibwa Sugar alisema ugumu walioupata kuifunga timu hiyo, inaonyesha jinsi atakavyokwenda kukabiliana na upinzani mkali kwenye ligi. “Tanzania kuna timu nzuri si Simba pekee, lazima tujipange ili kutetea ubingwa wetu, tunaanza ligi tukijua tunakwenda kukabiliana na wapinzani wenye timu nzuri,” alisema Aussems. Nao Prisons wanaingia katika mchezo huo wakiwa wametokea kambini visiwani Zanzibar walikokaa kwa wiki mbili na kucheza mechi nne za kirafiki. Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons,  Abdallah Mohammed, alisema wamejipanga kuondoka na pointi tatu katika mchezo huo kutokana na  maandalizi bora ya timu yao. “Siwezi kujua wapinzani wangu wamejiandaa vipi, kila kocha ana mbinu zake za kukabiliana na mchezo muhimu kama huu, kwa sisi lengo letu ni matokeo mazuri,” alisema Mohammed. Michezo mingine inayotarajiwa kupigwa leo, Singida United watawakaribisha Biashara United kutoka mkoani Mara katika Uwanja wa Namfua, Singida. Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Ndanda FC, Uwanja wa Mabatini, uliopo Mlandizi, Pwani, wakati Lipuli ya Iringa watakuwa wageni wa Coastal Union katika dimba la Mkwakwani, Tanga. Mechi nyingine Alliance na Mbao zote za jijini Mwanza, zitamenyana kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza huku Kagera Sugar wakiwakaribisha Mwadui FC katika Uwanja wa Kaitaba,  mjini Bukoba, mechi zote zikichezwa saa 10:00 jioni. Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo minne ambapo Yanga watacheza dhidi ya Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Azam FC watawakaribisha Mbeya City,  Uwanja wa Azam Complex, Chamazi,  Stand United watachuana na African Lyon, Uwanja wa Kambarage,  Shinyanga, wakati JKT Tanzania itakuwa mwenyeji wa KMC kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam.
4
    NA GUSTAPHU HAULE UTAFITI wa viashiria vya maambukizi ya virusi vya Ukimwi umeanza mkoani Pwani huku kaya zilizoainishwa kufanyiwa utafiti huo zikitakiwa kutoa ushirikiano ili ukamilike kwa wakati. Meneja Takwimu wa Mkoa wa Pwani, Kalisto Lugome, alikuwa akiwaeleza waandishi wa habari jinsi utafiti huo utakavyotekelezwa.   Lugome alisema  Mkoa wa Pwani umepata kipaumbele  cha kufanyiwa utafiti huo kutokana na kuwapo idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi yaliyofikia asilimia 7.2 wakati wastani kwa taifa ni asilimia tano. Alisema utafiti huo utafanyika katika halmashauri zote za mkoa  katika kaya 37 zilizoanishwa. Lugome alisema hivi  sasa timu ya wahamasishaji  imeanza kupita katika maeneo hayo   kufanya maandalizi. “Utafiti wa viashiria vya maambukizi ya virusi vya Ukimwi sasa umeingia mkoani kwetu. “Tunawaomba wananchi katika kaya zilizoanishwa kutoa ushirikiano  kuweza kukamilisha hatua hiyo kwa wakati,” alisema.   Awali akizindua hatua hiyo,  Mkuu wa Mkoa wa Pwani,   Evarist Ndikilo, alisema   utafiti huo utaisaidia Serikali hususan watunga sera, kuandaa mikakati mipya ya kudhibiti Ukimwi na kuimarisha mipango ya ufuatiliaji.  Ndikilo alisema takwimu hizo zitasaidia pia kuboresha juhudi zinazofanywa na Serikali kusogeza huduma za VVU katika vituo vya afya ikiwamo huduma ya mama kwenda kwa mtoto. Hata hivyo,  aliwataka waganga wakuu wa halmashauri hizo   na watendaji wote waweke  mazingira mazuri ya kuhakikisha watafiti hao wanafanya kazi yao kulingana na matakwa ya Serikali.  
3
BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro limeiomba Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuweka utaratibu wa kuwafuata wananchi katika ofi si za kata ili watoe huduma, badala ya wananchi kuwafuata ofi sini kwao na kusababisha usumbufu.Ombi hilo limetolewa kwa niaba ya baraza hilo na Diwani wa Viti Maalumu, Hadija Kibati (CCM), alipouliza swali la papo kwa papo juzi kwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo, John Mgalula ili atoe ufafanuzi kuhusu vitambulisho vya taifa. Kibati alisema wananchi wanatakiwa kuvitumia vitambulisho vya taifa kwenye usajili wa laini za simu ambalo limeanza jana hadi Desemba 31, mwaka huu, ambao wananchi wenye simu wameingizwa kwenye mfumo huo.Alisema kwa sasa ofisi za Nida ziko nje ya Mji wa Morogoro hivyo wananchi wamekuwa wakitumia gharama kwenda kuulizia vitambulisho ama kupata ufafanuzi, huku wengine wakishindwa kumudu gharama za usafiri. Alisema licha ya vitambulisho hivyo kuwa ni muhimu, lakini bado idadi kubwa ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro hawajavipata. Ofisi za Nida Morogoro ziko eneo la Tungi nje kidogo ya mji huo.Akijibu hoja hiyo kabla ya maelezo ya mkurugenzi, Meya wa Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga alisema ni vema Nida ikawafuata wananchi kwenye maeneo waliyopo kama walivyofanya wakati wa kuwaandikisha, badala ya kutembea umbali mrefu kufuata ama kuulizia vitambulisho hivyo.Katika hatua nyingine, Diwani wa Kata ya Sabasaba, Mudhihir Shoo alitaka kujua kuwa ni lini kituo cha mabasi Msamvu kitamilikiwa na manispaa hiyo kwa asilimia 100, tofauti na ilivyokuwa kwa sasa ambako kituo hicho kinamilikiwa kwa ubia wa Manispaa na uliokuwa Mfuko wa Pensheni wa LAPF. Meya Kihanga ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Kituo cha Mabasi Msamvu alisema mchakato wa kukikabidhi kituo hicho kwa Manispaa ya Morogoro unaendelea kwa kuwa tayari Rais John Magufuli aliagiza mamlaka mbalimbali kushughulikia.
3
NAIROBI, KENYA STAA wa muziki nchini Kenya ambaye anatamani kuwa na watoto wengi zaidi, Esther Akoth ‘Akothee’, amempa zawadi ya gari Mazda CX-7 mtoto wake wa pili, Rue maarufu kwa jina la Celine Dion baada ya kutimiza miaka 19. Msanii huyo alimpa binti yake zawadi hiyo yenye thamani ya zaidi ya milioni 22, huku akimtaka kukataa zawadi na lifti kutoka kwa wanaume wakware. “Chukua funguo, nina uhakika unaweza kujigharamia mafuta na matengenezo madogo madogo kutokana na mshahara ninaokulipa unaotokana na matunzo na malezi mazuri unayowapa wadogo zako, tafadhali epuka zawadi kutoka kwa wanaume, epuka vinywaji na lifti za bure. “Hakuna mwanamume atakayekupa kitu bure, wakikupa ujue kuna siku watafuata malipo, kuwa mwenye mawazo huru sasa umepata usafiri wa kwenda nao shule, asante kwa kuwa binti mwema nakupenda,” aliandika Akothee kwa binti yake. Binti yake alipopata ujumbe huo naye akajibu: “Nilipoona hali hiyo sikuweza kujieleza kwa mshtuko…mama utabaki kuwa mama mwema, nitalipenda gari langu muda wote na pia sitapokea zawadi wala lifti kwa kuwa nina la kwangu, nakupenda mama.” Licha ya kutoa zawadi hiyo ya gari, zaidi ya Sh milioni 10 zilitumika katika sherehe hiyo ya binti huyo iliyofanyika Mombasa.
1
Magufuli ambaye ameahidi kukutana na wasanii angalau kila mwaka, pia amekubaliana na maombi ya kutaka haki ya ubunifu isisimamiwe na Chama cha Hatimiliki cha Tanzania (Cosota), kilicho chini Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji badala yake iwe chini ya wizara yenye dhamana ya wasanii.Alisema hayo jana kwenye hafla iliyokutanisha wadau mbalimbali walioshiriki kwenye kampeni zake za urais mwaka jana; Wengi wao wakiwa wasanii aliowahakikishia kuwa ameanza nao, atamaliza nao na hatawaacha.Akizungumzia wizi wa kazi za wasanii ikiwemo kusambaa kwa CD zisizo na stika, Rais Magufuli alisema kama ambavyo TRA imefanya kazi kubaini kontena zisizolipa kodi, alitaka ifanye hivyo pia kwa upande wa kazi hizo za wasanii. Utaratibu huo wa kubandika stika kwenye kila nakala ya kazi itakayosambazwa, ulifikiwa na serikali ikiwa ni hatua ya kupambana na wizi wa kazi za wasanii .Kuhusu Cosota, Magufuli aliwataka Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa pamoja na Waziri mwenye dhamana ya sanaa, Nape Nnauye, kuhakikisha mambo yanayohusu wasanii yanakuwa chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo .Alisema masuala ambayo hayahitaji kwenda kwenye Baraza la Mawaziri au bungeni, yafanyiwe kazi mara moja. Alimtaka Waziri Nape amwandikie Waziri Mkuu, ili mambo yaliyo kwenye mamlaka yake (Rais) ayafanyie kazi mara moja wasanii wanufaike na kazi zao.Cosota ilianzishwa kwa mujibu wa Sehemu ya 46 ya sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki Namba 7 ya mwaka 1999.“Nataka wasanii wafaidike na haki na ubunifu wao. Wamepewa vipaji na Mungu, haiwezekani mtu mwingine ndiye afaidi kazi yake,” alisema Magufuli.Awali, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye sanjari na baadhi ya wasanii, wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye hafla hiyo, walisema nchi imevamiwa na kazi nyingi kutoka nje ya nchi ikiwemo CD zisizokuwa na stika zikiuzwa kwa bei ya kutupa inayoathiri kazi za wasanii wa ndani.Waziri Nape alimuomba Rais Magufuli, ufanyike mchakato suala hilo la haki miliki za wasanii libaki kwenye wizara yake.Awali, wakimshukuru Magufuli kwa kuwaalika, baadhi ya wasanii, akiwemo mwigizaji, Jacob Steven ’JB’ na msanii wa komedi, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’, walisema baada ya uchaguzi, walibezwa kuwa Ikulu watabaki kuisikia redioni kwa maana hawawezi kualikwa.
4
WAZIRI wa Nchi Ofi si ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amesema uamuzi wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wa kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki, sio wa kushtukiza kwani wadau na wananchi walisubiri hilo.Lakini, amesisitiza kuwa marufuku hiyo haihusu vifungashio vya maziwa, chupa za maji, vifungashio vya madawa sekta ya kilimo (green houses) ujenzi na viwanda. Alisema badala yake utawekwa utaratibu wa kukusanya uchafu unaotokana na bidhaa zao. Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana jijini hapa, January alisema kauli ya Waziri Mkuu kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia Juni Mosi, mwaka huu sio wa kushtukiza na wananchi walikuwa na makalamiko juu ya matumizi ya mifuko hiyo kutokana na kuwa na athari kwenye mazingira.“Hata utafiti uliofanyika unaonesha ifikapo mwaka 2050 kutakuwa na plastiki nyingi kwenye bahari kuliko samaki,” alisema. Aliongeza kuwa kuanzia mwaka 1993, serikali ilianza kuchukuliwa hatua na ilipofika mwaka 2006 kukawa na viwango vya plastiki zinazoweza kutumika. Alisema kuanzia mwaka 2016 walianza kuchukuliwa hatua ili kupiga marufuku moja kwa moja na walifanya maandalizi kuhusu hatua hiyo kwa kuzungumza na wenye viwanda kuhusu dhamira ya serikali na Mei 2016 walitangaza dhamira hiyo.Alisema Agosti 24, 2016 Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI) waliandika barua kutaka katazo hilo lianze Desemba 31, 2017. “Tumetoa katazo hilo mwaka na nusu zaidi ya walivyoomba, mwaka 2017 tulikutana na wadau ukumbi wa Karimjee na wakatoa maoni na walisema kwa nini serikali inachelewa kutoa maamuzi, Pia Novemba mwaka jana tulifanya mkutano Ukumbi wa JK Nyerere, tulialika wadau wanaotengeneza mifuko mbadala tulihakikishiwa uwezo huo upo,” alieleza January. Alisema uamuzi huo sio wa kushtukiza na wadau, wana taarifa na kumekuwa na ushirikishwaji kwa wanaotengeneza mifuko mbadal na katazo hilo ni jambo ambalo wananchi walikuwa wanalidai kwa serikali.Alisema kuna wazalishaji wameanza kufanya biashara ya mifuko mbadala kama vikapu, mifuko ya karatasi na ile ya vitambaa na walikuwa wakisuburi tamko ili waanze uzalishaji. Alisema nchi za Kenya na Rwanda, zilishapiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki na wamekuwa wakinunua mifuko ya katarasi kutoka kiwanda cha Mgololo. “Kama kiwanda cha Mgololo kinaweza kupeleka mifuko Kenya na Rwanda hawawezi kushindwa kuzalisha mifuko kwa ajili ya Tanzania,” alihoji. Alisema hatua ya kwanza ni kuandika kanuni za katazo rasmi na la kisheria na litakuwa na nguvu za kisheria. Alisema zitawekwa adhabu kwa wanaoagiza, kutengeneza, kukutwa nazo kwenye ghala na dukani.Adhabu zitawekwa kulingana na ukubwa wa kosa. Alisema vifungashio vya plastiki ambavyo havipigwi marufuku ni vifungashio vya dawa sekta ya kilimo, sekta ya viwanda, ujenzi. Pia vifungashio ambavyo bidhaa zake muhimu zinatumika kuhifadhia vitu kama maziwa. Sekta hizo lazima ziwekewe utaratibu utakaowezesha kukusanya uchafu unaotumika na bidhaa zao. “Chupa za plastiki hazipigwi marufuku, tutaweka utaratibu wa kukusanya,” alisema.Aliongeza kuwa kitaundwa kikosi kazi cha serikali kusimamia katazo hilo cha wataalam kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Uhamiaji, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Makamu wa Rais na Tamisemi. “Suala la kupiga marufuku matumizi ya plastiki linafanyika kwa dhamira njema na wanaoingiza mifuko hiyo wataona jambo hilo ni gumu na halifai,” alisema. Alisema asilimia 80 ya mifuko ya plastiki iliyokuwa ikitumika nchini, haitengenezwi Tanzania.
3
Shirika la ndege la Precision Air limesaini mkataba wa ushirikiano na Hospitali ya CCBRT ili kuboresha huduma kwa watu wenye ulemavu nchini. Kutokana na makubaliano hayo, shirika hilo litatoa tiketi za ndege 120 kwa hospitali hiyo kwa ajili ya kuwezesha shughuli zake za kliniki za matibabu mikoani pamoja na shughuli za kiutawala. Akizungumza kwenye hafla ya kuweka saini mkataba huo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Patrick Mwanri amesema ushirikiano huo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora za afya.“Tunaelewa kwamba kuna vikwazo vingi vinavyozuia watu wanaoishi na ulemavu kusafiri kutoka mikoa mbalimbali kuja Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu, ndiyo maana tumashirikiana ili kwamba huduma hizi za kliniki ziwafikie huko waliko,” ameeleza. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa CCBRT, Brenda Msangi, asasi hiyo ina vituo washirika kwenye mikoa mbalimbali, hivyo watoa huduma wake wataweza kufikia watu wengi zaidi wenye uhitaji wa huduma kama za macho, mifupa, vipimo, ugawaji wa baiskeli kwa ajili ya walemavu na nyinginezo.
3
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa Yanga, George Lwandamina, bado anahaha kuisuka safu yake ya ushambuliaji ili kuhakikisha inafunga mabao ya kutosha. Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, walianza msimu mpya kwa kusuasua baada ya kulazimisha sare ya 1-1 na Lipuli katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Katika mchezo huo, Lipuli inayofundishwa na kiungo wa zamani wa Simba, Seleman Matola, ilionesha kiwango maridadi huku ikifanikiwa kufunga bao la kuongoza kabla ya Yanga kusawazisha. Kabla ya sare na Lipuli, Yanga ilichapwa na Simba penalti 5-4 katika pambano la Ngao ya Jamii baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 kwa suluhu. Katika mazoezi yaliyofanyika jana kwenye Uwanja wa Uhuru, Lwandamina alionekana akitilia mkazo katika kuwapika washambuliaji wake pamoja na kuimarisha safu yake ya ulinzi. Lwandamina alikigawa kikosi chake katika makundi matatu, kila moja likiwa na washambuliaji wanne na mabeki wanne. Kwa upande wa washambuliaji walitakiwa kuchukua mpira katikati ya uwanja na kuingia nao eneo la hatari ambako walikutana na mabeki na kutakiwa kutafuta mbinu za kuwapita na kufunga mabao. Hata zoezi hili halikuhusu kundi zima, badala yake lilifanyika kwa utaratibu wa mshambuliaji mmoja kutakiwa kumvaa  beki mmoja. Kundi la kwanza la washambuliaji lilikuwa Donald Ngoma, Ibrahim Ajib, Yusuph Mhilu na Matheo Antony, wakati Abdallah Shaibu, Juma Abdul, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Haji Mwinyi, walikuwa mabeki. Kundi la pili liliundwa na Emmanuel Martin, Juma Mahadhi, Said Juma na Pius Buswita, wakati mabeki wakiwa Andrew Vincent, Kessy Ramadhani na Pato Ngonyani. Kundi la mwisho alikuwepo Kabamba Tshishimbi, Thaban Kamusoko, Said Juma na Maka Edward, huku Ninja, Abdul, Cannavaro na Mwinyi wakiunda timu ya mabeki. Akizungumza baada ya mazoezi hayo, Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, alisema baada ya sare yao na Lipuli wamekuwa wakifanyia maboresho kikosi chao ili kuhakikisha wanapata ushindi dhidi ya Njombe Mji. Alisema licha ya baadhi ya wachezaji kuitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars hali hiyo haitawaathiri kwa kuwa bado wana hazina kubwa ya wachezaji. “Nafahamu tunakabiliwa na michezo ya ugenini, ukizingatia awali tulicheza na timu ambayo imepanda daraja na mechi inayofuata na wao vile vile ni wageni na wameweza kuonyesha uwezo mzuri,  tunatakiwa tukapambane kwa ajili ya kuhakikisha tunapata pointi tatu. “Kimsingi kila unapocheza mechi moja unajiuliza kuhusu inayofuata, ndivyo mpira ulivyo, jambo la msingi tunawaomba mashabiki wa Yanga waendelee kutuunga mkono kwa kuwa  hii ni vita na kila mmoja anataka kushinda,” alisema Nsajigwa.  
4
RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amesema kutokana na juhudi kubwa za serikali za kuimarisha uchumi, ukusanyaji wa mapato umeongezeka na kwamba kwa mwaka 2017/18 serikali ilikusanya Sh bilioni 688.7 ikilinganishwa na Sh bilioni 521.8 zilizokusanywa na taasisi za ukusanyaji kodi kwa mwaka 2016/17.Taasisi zinazokusanya kodi kwa ajili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ni mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) na Bodi ya Mapato ya Zanzibar (ZRB).Akihutubia maelfu ya wananchi waliofurika katika Uwanja wa Gombani, Chakechake kisiwani Pemba jana kuhitimisha kilele cha miaka 55 ya Mapinduzi, Dk Shein alisema kwamba kasi ya ukuaji wa uchumi imefikia asilimia 7.7 kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 5.8 kwa mwaka 2016.Kadhalika alisema pato la mtu binafsi liliongezeka na kufikia Sh milioni 2.1 sawa na dola za Marekani 944 kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na Sh milioni 1.89 sawa na dola za Marekani 868 kwa mwaka 2016, huku mfumuko wa bei ukiendelea kudhibitiwa katika tarakimu moja.Kwa mwaka 2018 kasi ya mfumuko wa bei ilifikia asilimia 3.9 ikilinganishwa na asilimia 5.6 katika mwaka 2017.Utegemezi Aidha, Dk Shein alisema kwamba mafanikio ya ukuaji wa uchumi kumeifanya serikali yake kupunguza hali ya utegemezi wa bajeti ambao kwa sasa umefikia asilimia 5.1 kwa mwaka 2018/20219 ikilinganishwa na utegemezi wa asilimia 7.3 kwa mwaka 2017/18.“Wakati serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, awamu ya saba inaingia madarakani mwaka 2010/11 kiwango cha utegemezi kilikuwa ni asilimia 30.2,” alisema Dk Shein na kuongeza kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na juhudi mbalimbali za serikali ikiwemo kuwashajiisha wazalishaji wa ndani na kuweka mazingira mazuri ya biashara katika uagizaji na usafirishaji wa bidhaa nje ya Zanzibar.Aidha alisema kwamba serikali yake imeendelea kuimarisha sekta ya viwanda na mchango wake katika pato la taifa umefikia shilingi bilioni 631.6 sawa na asilimia 19.6 kwa mwaka 2017, kutoka shilingi bilioni 528.6 mwaka 2016 sawa na asilimia 19.2 na kuongeza kuwa hilo limechangiwa na kuimarika kwa viwanda mbalimbali vilivyopo Zanzibar.Kwa upande wa biashara kati ya Zanzibar na Tanzania Bara, alisema jumla ya bidhaa zenye thamani ya Sh bilioni 17.21 zilisafirishwa kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara na bidhaa zenye thamani ya Sh bilioni 232.59 zilisafirishwa kutoka Tanzania Bara kuja Zanzibar.Uinuaji wa pato la watuKatika kuinua pato la mtu mmoja mmoja, Rais Shein alisema kwamba kwa miaka saba mfululizo serikali yake imeendelea kutekeleza sera yake ya kumlipa mkulima kiwango cha asilimia 80 ya bei ya karafuu katika soko la dunia ambayo ni sawa n ash 14,000 kwa kilogramu moja.Hata hivyo, alisema kwamba jumla ya tani 7,464 za karafuu zenye thamani ya Sh bilioni 131.955 zimeuzwa nje ya nchi kwa mwaka 2017/18 ikilinganishwa na tani 2,253 za karafuu zenye thamani ya Sh bilioni 38 zilizouzwa mwaka 2016/17.Pia alisema lipo ongezeko la pato kutokana na utalii kuongezeka kwa idadi yao kila mwaka na kuwa kwa mwaka 2018 jumla ya watalii 520,809 waliwasili nchini ukilinganisha na watalii 433,116 waliwasili mwaka 2017.Aidha alisema wataendelea na kujitangaza pamoja na kufanya maonesho kila mwaka ya utalii ili kuvutia watalii zaidi.Akizungumzia mafanikio mengine mengi ya mapinduzi alisema kwamba serikali yake imeyaishi malengo ya mapinduzi kwa kusogeza huduma nzuri na bora kwa wananchi.Huduma hizo ni katika sekta ya maji, elimu, uchukuzi na utetezi wa wanyonge hasa watoto na wanawake.ElimuAlisema katika hotuba yake hiyo kwamba miongoni mwa malengo makuu ya mapinduzi yalikuwa ni kuwapa elimu bila malipo na yenye manufaa wananchi wake kwa ajili ya maisha yao na kwamba katika kipindi cha miaka 55 ya mapinduzi yamepatikana mafanikio makubwa sana na kuimarika kwa huduma za elimu.“Kabla ya mapinduzi ya mwaka 1964 huduma hizo zilikuwa chache na zikitolewa kwa ubaguzi na wachache waliopata fursa ya elimu, walilazimika elimu hiyo wailipie” alisema na kuongeza kwa idadi ya shule zilikuwa chache lakini kwa sasa zipo nyingi na elimu inatolewa bure toka awali msingi hadi sekondari na wale wanoafika chuo kikuu wanasomeshwa kwa mkopo.Alisema siku za maandalizi zimeongezeka kwa mara 272 zenye wanafunzi 72,151 kwa mwaka 2018 ukilinganisha na skuli mbili zilizokujwa na wanafunzi 60 kwa mwaka 1963.Upande wa sekoindrai nao umeongezeka mara 67 kufikia junmla ya shule 268 zenye idadi ya wanafunzi 126,913 kwa mwaka 2018 ikilinganishwa na skuli 4 zilizokuwa na idadi ya wanafunzi 734 kwa mwaka1963.AfyaAlisema serikali inaendelea na uamuzi wake ilioutoa Machi 3,1965 wa kuwapa wananchi matibabu bure na huduma zake zinaendelea kuimrishwa kwa kuajiri wataalamu zaidi, kujenga hospitali kupandisha hadhi zilizopo na kuhakikishakwamba wahudumu wanakuwa na nafasi ya kusikiliza wagonjwa wao kwa kupunguza kiwango cha uwiano kati ya wahudumu na wagonjwa.Rais Shein alisema kutokana na juhudi hizo kiwango cha malaria kimepungua na kubaki asilimia 0.4 mwaka 2018.Pamoja na mafanikio alisema kwamba taifa hilo linachangamoto ya maradhi yanayoambatana na kuimarika kwa uchumi wa wananchi kama kisukari,maradhi ya moyo ambayo mengi yanatokana na kubadilika kw atabia za ulaji.Kuhusu tatizo la dawa alisema litaisha kwa sababu wametanua bajeti ya wizara ya afya kwa kutenga Sh bilioni 12.7 ikilinganishwa na Sh bilioni 7.0 mwaka 2017/18.MajiDk Shein amesema kwamba ni jambo la kufurahishwa kwamba hivi sasa vijiji mbalimbali vya mkoa wa Kaskazini Unguja vinaendelea kupata maji safi na salama baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji uliotekelezwa na kampuni ya First Highway Engneering of China ; huku upande wa pemba huduma za maji safi na salama zinapatikana kw akiwango cha kuridhisha.Kilimo Katika kuimarisha kilimo cha umwagiliaji cha mpunga, miundombinu ya umwagiliaji katika hekta 1,524 kwenye bonde la Cheju, Bumbwisudi na Kibokwa kwa Unguja na bonde la Makwararani na Chamanangwe kwa Pemba zitajengwa na mkandarasi kutoka Korea na mkataba umeshatiwa saini.Aidha mpango wa maendeleo ya sekta ya kilimo utakaogharimu dola za Marekani milioni 148 utaketelezwa kwa muda wa miaka 10 kwa v ipindi viwili vya miaka mitatu mitatu na kipindi kimoja cha miaka mine.MiundombinuAlisema serikali inaendelea na ujenzi wa barabara kuu na barabara za ndani unguja na Pemba. Alisema kuwa baadhi ya bara zimekamilika na nyingine zinaendelea kujengwa huku zingine zikitafitiwa fedha.Pia alisema kwamba juhudi zinaendelea kuhakikisha kwamba ujenzi wa jengo la abiria uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume unakamilika na fedha za kujenga bandari mpya ya Mpigaduri zinapatikana na ujenzi unaanza mwaka huu.Uwezeshaji Aidha alisema serikali yake inaendelea kuwawezesha wananchi kiuchumni na kupambana na tatizo la ajira na kuongeza kuwa mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi utaendelea kuimarishwa ili kutoa mikopo zaidi kwa wananchi.Kwa mwaka 2018 alisema mikopo 451 yenye thamani ya Sh milioni 685 imetolewa kwa wajasiriamali wa Unguja na Pemba.
3
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM CHAMA cha Wakunga Tanzania (TAMA), tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, kimepanga kutoa huduma ya upimaji wa saratani ya kizazi na satarani ya matiti bure kwa wanawake. Hayo yalielezwa jana na Mwenyekiti wa TAMA – Muhimbili, Priscilah Kinyamagoha kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo mwenyekiti huyo alisema upimaji huo utafanyika Agosti 4, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Duniani. “Pamoja na huduma hizo, pia tutafanya upimaji wa shinikizo la damu, sukari, uzito na urefu, upimaji wa virusi vya ukimwi kwa hiyari, ushauri kuhusu lishe bora, ushauri kuhusu uzazi wa mpango, elimu juu ya unyonyeshaji sahihi kwa watoto chini ya umri wa miaka miwili na elimu juu ya afya ya kinywa na meno,” alisema. Alisema TAMA itafanya upimaji huo kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI). “Ikumbukwe kwamba Mei 5, mwaka huu huwa tunaadhimisha Siku ya Wakunga Duniani, lakini TAMA tulisogeza mbele maadhimisho hayo hivyo tutafanya Agosti 5, mwaka huu na tutatoa huduma hizo nilizozitaja,” alifafanua.
3
Taarifa ya Vodacom kwa vyombo vya habari, ilifafanua jana kuwa, huduma hizo kwa sasa zimeanza kutolewa katika duka la Uchumi lililopo katika jengo la Quality Center jijini Dar es Salaam.Vodacom pia imefungua duka la huduma kwa wateja wake ndani ya duka hilo, ikiwa ni ubunifu wa aina yake hapa nchini na hivyo kuwapa nafasi ya kipekee wateja wa Vodacom kumaliza mahitaji yao yote kwa nwakati mmoja “Tunazidi kuongoza katika ubunifu, hili ni jambo tunalolipa kipaumbele kwa lengo la kuhakikisha tunatoa nafasi kwa wateja wetu kufaidi matumizi ya teknolojia na kubadili maisha yao, hakuna shaka kila tunachokifanya kinatimiza matarijio ya wateja wetu.“Kila mmoja wakati huu wa msimu wa sikukuu, angependa kutumia muda mfupi na kwa urahisi zaidi kupata huduma, hatua moja muhimu ni kuwawezesha kuwa na njia rahisi na nyepesi zaidi ya kukamilisha mahitaji yao na hivyo ndivyo tunavyofanya leo kwa kuwatangazia wateja wetu kutumia M-pesa wanapofika duka la Uchumi,” taarifa hiyo ilieleza.Kwa sasa M-Pesa inawaunganisha wateja wa Vodacom na biashara zaidi ya 300 katika nyanja mbalimbali ikiwemo kulipia tiketi za ndege, ving’amuzi, Luku, maji, kutoa na kuweka fedha katika akaunti za benki zaidi ya 20 na hivyo kuongoza soko miongoni mwa huduma za fedha kwa njia ya simu.Meneja Mkazi wa duka la Uchumi, Chriss Lenana alisema ni jambo la furaha na kujivunia kuzinduliwa kwa ubia huo kati ya kampuni yake na Vodacom na kuwawezesha wateja wake kutumia simu zao kwa malipo ya ununuzi.“Kufunguliwa kwa duka la Vodacom hapa kwetu kutasaidia sana wateja wetu si tu kuweza kupata huduma za M – PESA bali pia huduma nyingine za kimawasiliano na hatimaye kuepukana na matatizo ya kimawasiliano yanayowakabili.Tunapokea idadi kubwa ya wateja kila kukicha na kwa kufunguliwa kwa duka hili Vodacom wamefanya suala la msingi ambapo awali iliwalazimu wateja kusafiri mpaka makao makuu kufuata huduma hizo kitu ambacho ni usumbufu na kiusalama ni changamoto,” alisema Lenana.“Huduma hii ya malipo kwa njia ya M-Pesa tutaisamabza kwenye maduka yetu yote ambayo yapo kwenye mipango yetu ya mwaka 2014/2015, ni wazi tumewaptia wateja wetu kitu kizuri na tunawaomba watumie njia hii ya malipo kwa kujiamini kwani mteja hupatiwa pia stakabadhi ya mununizi”Aliongeza Duka hilo ni moja ya maduka 200 ya Vodacom ambayo yapo mbioni kufunguliwa nchi nzima na pia ni muendelezo wa uboreshwaji wa huduma ya M-Pesa na huduma nyinginezo za kampuni hiyo nchi nzima.
5
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) imesisitiza nia yake ya kupambana na misumeno ya moto kwa kuiteketeza ili kupunguza athari za kimazingira za ukataji wa miti kiholela.Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mihayo Juma Nhunga wakati akijibu swali la mwakilishi wa jimbo la Chakechake, Suleiman Sarhani aliyetaka kujua mikakati ya kudhibiti misumeno ya moto zimefikia wapi kwa sasa.Nhunga amesema serikali kupitia Idara ya Misitu na Mali zisizorejesheka imetangaza rasmi kupiga marufuku misumeno ya moto nchini kote baada ya kubainika kuwepo kwa kasi ya ukataji wa miti ikiwemo ya matunda.Amesema tayari serikali imetoa muda wa mwezi mmoja kwa wamiliki wa misumeno ya moto kuisalimisha katika taasisi husika ikiwemo kwa viongozi wa shehia pamoja na Jeshi la Polisi.Aliwataja masheha wa shehia zote za Unguja na Pemba kuhakikisha wanawafichua watu wanaomiliki misumeno ya moto katika maeneo yao kwa sababu wanafahamika.''Serikali tayari imetoa agizo la kukamatwa kwa misumeno ya moto nchini kote ambapo watu wanaoimiliki wametakiwa kuipeleka kwa viongozi wa shehia ikiwemo masheha na serikali za halmashauri ya wilaya na mikoa,'' alisema.Alizitaja sababu kubwa za serikali kupiga marufuku misumeno ya moto ni tishio la uharibifu wa misitu pamoja na ukataji wa miti ya matunda ikiwemo Minazi na Miembe.Alisema katika kipindi cha miaka miwili, kumejitokeza wimbi kubwa la ukataji wa miti ikiwemo minazi kwa ajili ya matumizi ya mbao huku misumeno ya moto ikitumika kufanya kazi hizo.Hivi karibuni katika sherehe za maonesho ya kilimo zilizofanyika Pemba, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein alitangaza rasmi kupigwa marufuku kwa misumeno ya moto na watu wanaoimiliki wametakiwa kuisalimisha katika taasisi husika.
3
Ushauri huo ulitolewa kutokana na mapango ya utalii ya Amboni mkoani hapa, kutopata watalii wengi. Aidha, imeelezwa taarifa zilizohusisha mapango hayo ya utalii na tukio la uhalifu la hivi karibuni, ziliathiri ujio wa watalii katika mapango hayo licha ya kwamba matukio husika, yalijitokeza eneo tofauti na eneo hilo.Akitoa maelezo juzi kwa watalii waliotaka kufahamu hali ya ujio wa wataalii kutembelea eneo hilo, Mhifadhi wa Mambo ya Kale wa Mapango ya Amboni, Jumanne Gekora, alisema watalii 65 wa ndani na mmoja wa nje mmoja hutembelea mapango hayo kwa mwaka.Miongoni mwa watalii waliofika eneo hilo juzi, ni timu ya wadau na wataalamu wa Muungano wa Utepe Mweupe Tanzania (WRATZ) ambao walitembelea vituo vyote 13 vilivyo ndani ya pango kuu kushuhudia vivutio vilivyomo.Mhifadhi huyo alisema eneo hilo la kitaifa la utalii, halitangazwi na kunadiwa kama ilivyo maeneo mengine ya utamaduni yaliyo chini ya dunia kama vile Mji Mkongwe wa Zanzibar, Bagamoyo na Olduvai Gorge pamoja na mbuga za wanyama.
5
Mwandishi Wetu LEO inatarajiwa kuwa siku ya mwisho ya utumishi jeshini kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange. Jenerali Mwamunyange ambaye alizaliwa mwaka 1959, alikuwa amalize muda wake Januari 30, mwaka jana, lakini Rais Dk. John Mgufuli alimwongezea mwaka mmoja wa utumishi jeshini. Mwamunyange ambaye ni Mkuu wa Majeshi wa saba tangu jeshi hilo lianzishwe mwaka 1964, ametumikia nafasi hiyo kwa miaka tisa na mienzi minne sasa. Wengine ni majenerali wastaafu, Mrisho Sarakikya (1964-1974), Abdallah Twalipo (1974-1980), David Musuguri (1980-1988), Ernest Kiaro (1988-1994), Robert Mboma (1994-2002), George Waitara (2002- 2007). Januari 30 mwaka jana, akizungumza na waandishi wa habari  makao makuu ya JWTZ (Ngome) Upanga, Dar es Salaam, Jenerali Mwamunyange alisema. “Mimi mwenyewe ilikuwa nistaafu kazi leo tarehe 30 Januari 2016, lakini Rais na Amiri Jeshi Mkuu ameamua kunibakiza katika utumishi jeshini kwa mwaka mmoja kuazia leo tarehe 30 Januari, 2016 hadi tarehe 31 Januari 2017,” alisema. Jenerali Mwamunyage alisema sababu iliyomfanya Rais Dk. Magufuli kumwongezea muda huo, imetokana na kutopata mtu sahihi wa kujaza nafasi hiyo. Pia Oktoba 30, mwaka jana akiwa kwenye kilele cha sherehe za miaka 52 ya kuanzishwa kwa JWTZ zilizofanyika Bagamoyo mkoani Pwani, Rais Dk. Magufuli alimwahidi Mwamunyange kumpa kazi nyingine baada ya kustaafu kwake. "Watu wameanza kusema nataka 'kuimilitarize' Serikali (kuendesha serikali kijeshi), lakini ukweli ni kwamba wanajeshi wana sifa nzuri ya maadili na uchapa kazi na hata wewe Mkuu wa Majeshi (Mwamunyange), ukistaafu nafasi zipo za kufanya kazi," alisema Rais Magufuli. Rais Magufuli alisema anapenda kuteuwa wanajeshi katika nafasi mbalimbali serikalini kwa sababu anasukumwa na upendo wake kwao kutokana na sifa walizonazo za kuwa na maadili na kuchapa kazi. Baadhi ya maofisa wa JWTZ waliotafutwa jana ili kuzungumzia suala hilo, walisema jambo la kustaafu ama kutostaafu kwa Mkuu wa Majeshi lipo katika mamlaka ya Rais. Taarifa nyingine zimedai kuwa takribani wiki moja sasa kumekuwa na shughuli katika kambi mbalimbali za jeshi Dar es Salaam za kumpongeza Jenerali Mwamunyange kutokana na utumishi wake jeshini. Kabla ya Mamunyange kuteuliwa kushika wadhifa huo na Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete Septemba 2007, alimpandisha kutoka cheo cha Luteni Jenerali kuwa Jenerali na kumteua kuwa Mkuu wa Majeshi. Kabla ya uteuzi huo, Mwamunyange alikuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ. Januari mwaka jana, alipokuwa akitangaza kuongezewa muda, alitangaza pia mabadiliko yaliyofanywa na Rais Magufuli jeshini. Mabadiliko hayo ilikuwa ni pamoja na kuwateua, Luteni Jenerali Venance Mabeyo kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Meja Jenerali James Mwakibolwa  kuwa Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu, ambapo kabla alikuwa Mkuu wa Tawi la Utendaji wa Kivita na Mafunzo Makao Makuu ya Jeshi. Jenerali Mwamunyange, alimtaja pia  kamanda mwingine aliyeteuliwa na Rais ni Meja Jenerali Yakub Sirakwi kuwa  Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa (Commandant NDC) kuchukua nafasi ya Meja Jenerali Gaudence Milanzi ambaye ameteuliwa na Rais kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii. Meja Jenerali Sirakwi alikuwa Mratibu Msaidizi Mkuu Baraza la Usalama wa Taifa- BUT.   JWTZ ilivyong’ara Ndani ya miaka tisa ya Jenerali Mwamunyage, JWTZ imefanya kwa mafanikio shughuli mbalimbali za kulinda amani katika mataifa yenye vita pamoja na operesheni nyingine za kupambana na  waasi wakiwamo wa Kundi la   M23  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Mwaka 2008, Majeshi ya Umoja wa Afrika yaliyoongozwa na JWTZ kwa kushirikiana na Jeshi la Shirikisho la Comoro, yalifanikiwa kukikomboa kisiwa cha Anjouan kwenye operesheni ambayo haikupata upinzani. Operesheni hiyo, iliyopewa jina la `Demokrasia Comoro’ ilifanya Kanali Mohamed Bakar aliyekuwa akikiongoza kisiwa hicho kimabavu baada ya kujitangazia utawala mwenyewe Julai, 2007, kutorokea  kisiwa cha Mayotte kilichopo chini ya utawala wa Ufaransa. Tangu mwaka 2009, JWTZ imekuwa ikipeleka wanajeshi wa kulinda amani Darfur nchini Sudan, shughuli ambayo inaelezwa kwamba imefanywa kwa weledi mkubwa. Msemaji wa JWTZ, Meja James Macheta alipoulizwa kustaafu kwa Jenerali Mwamunyange, alimtaka mwandishi wetu kuwa na subiri kwa kile alichodai yuko barabarani anaendesha gari. 
3
MPANGO wa Tathmini ya Utawala Bora katika Bara la Afrika (APRM), umebaini kuwepo kwa mafanikio makubwa nchini Tanzania, kwa kuimarisha demokrasia, usimamizi wa uchumi na huduma jamii.Pia mpango huo unatajwa kufanya vyema katika maeneo mengine, yakiwemo ya uendeshaji wa mashirika ya biashara, ambako zaidi Tanzania inasifiwa katika eneo la usimamizi wa rasilimali ya ardhi na madini.Akizungumza wakati wa mkutano wa wadau kutathimini mpango huo, ulioanzishwa miaka 16 iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi alisema mpango huo umeonesha Tanzania kuwa na mafanikio makubwa katika usimamizi wa utawala bora. Profesa Kabudi alisema mafanikio hayo yanatokana na umoja na ushirikiano uliopo baina ya wananchi wa Tanzania na viongozi wa serikali, hatua iliyoiwezesha kuwa moja ya nchi zilizofanya vizuri.“Tanzania kwa miaka mingi tumekuwa na utawala bora, ni juhudi zilizofanywa na Rais Magufuli nasi tunaziendeleza, mafanikio haya yanatokana na juhudi zetu wenyewe kama serikali chini ya uongozi madhubuti,” alisema Profesa Kabudi. Alisema tathmini hiyo ya miaka 16, imeangalia pia maeneo mengi muhimu yakiwepo ya huduma za jamii za elimu bure, maji, afya ikiwepo ujenzi wa zahanati na upatikanaji wa huduma za afya.Mtaalamu wa masuala ya kutathmini utawala bora kutoka APRM, Dk Rehema Twalib alisema Tanzania imekuwa ni nchi ya mfano kwenye maeneo ya demokrasia baada ya kuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, uchumi, sera na mipango mizuri, na kwenye eneo la biashara ikiwepo kwenye sekta binafsi.Dk Twalib alisema katika kufanikisha mpango huo, Tanzania imepiga hatua kubwa kiasi cha kuiwezesha kutambulika miongoni kwa nchi 33 zinazotekeleza mpango huo Afrika. APRM ni Mpango wa tathmini ya utawala bora katika Bara la Afrika, wenye lengo la kuangazia nchi hizo na kufanya tathmini kwenye masuala mbali mbali ya huduma za jamii.
3
LIGI Daraja la Kwanza imezidi kuchanja mbuga ikimalizika mzunguko wa sita, huku timu zikionesha ushindani mkubwa. Katika Kundi A, Mawenzi Market inaongoza ikiwa na pointi 10 sawa na Mlale FC, Namungo FC na Mbeya Kwanza zikitofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa. Friends Rangers na Majimaji FC zina pointi tisa kila moja, Mufindi United ina pointi nane, Reha FC ina pointi saba, Ashanti United ina pointi sita, Kiluvya United ina pointi tano, Njombe Mji ina pointi nne na Dar City ina pointi tatu. Pamba FC inaongoza Kundi B ikiwa na pointi 11, sawa na timu za Boma FC na Arusha United, lakini zikitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.Geita Gold na Rhino Rangers zina pointi 10 zikitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa, Polisi Tanzania ina pointi tisa, Green Warriors na Dodoma FC zina pointi nane nazo zikitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.Transit Camp ina pointi saba, Mashujaa FC ina pointi sita, Arusha FC ina pointi tatu na Mgambo Shooting ina shika mkia ikiwa na pointi mbili. Kila timu itakayokuwa inashika nafasi ya kwanza itapanda Ligi Kuu moja kwa moja, huku mshindi wa pili akichezeshwa pamoja na timu, ambazo zitashika nafasi ya 17 na 18 katika Ligi Kuu baada ya msimu kumalizika ili kupata timu mbili zitaungana na mshindi wa kwanza wa kila kundi kupanda Ligi Kuu.
4
MBUNGE wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) amesema ni aibu Tanzania kuchukua makocha kutoka nje huku kukiwa na wazawa wenye uwezo mkubwa.Akichangia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa mwaka 2018-2019, Nkamia alisema ni aibu kwa kocha wa mpira wa miguu kutoka Burundi. “Ni aibu kocha wa mpira wa miguu kutoka Burundi huku wazawa wakiwa hawapewi nafasi,” alisema.Nkamia aliyewahi kuwa kiongozi kwenye klabu ya Simba miaka ya nyuma alisema pia kwa sasa Ligi ya Soka ya Wanawake na Ligi Kuu imekuwa mahututi kutokana na timu kulia njaa. “Hata Ligi ya Wanawake hali sio nzuri, mfano timu inatoka nyumbani na ugenini timu inatoka Njombe haina hata sehemu ya kulala kwa sababu ya ukata, hatuwezi kuendesha mpira hivyo.”Kutokana na kauli hiyo, Spika Job Ndugai alisema: “Mheshimiwa Nkamia, sio timu za kina dada tu hata timu fulani zinatembeza bakuli mheshimiwa Nkamia.” Katika hatua nyingine, Mbunge wa Konde Khatibu Said Haji (CUF) amehoji ni kiasi gani cha fedha ambacho kimekuwa kinatolewa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) kwa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA).Akiuliza swali jana bungeni, Haji alihoji: “FIFA inatoa misaada ya fedha kwa kupitia TFF. Je, ni kiasi gani cha fedha TFF imekuwa ikiipatia Zanzibar kupitia ZFA?” Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza alisema ni kweli FIFA inatoa msaada wa fedha kwa mashirikisho ya mpira wa miguu ikiwemo TFF kwa ajili ya miradi na programu mbalimbali.Alisema fedha hizo huwa ni maelekezo maalum kwa lengo la kusaidia na kuendeleza maeneo ya Ligi ya Wanawake, Vijana pamoja na masuala ya kiutawala. “Kuanzia mwaka huu FIFA itakuwa inatoa jumla ya dola za Marekani milioni 1.25 kila mwaka kwa wanachama wake ikiwemo ZFA ambayo ni sehemu ya TFF,”alisema. Akifafanua mchanganuo wa fedha hizo, Shonza alisema fedha za miradi kiasi cha dola za Marekani 750,000, fedha kwa ajili ya kuendesha ofisi dola za Marekani 500,000.“Hata hivyo kwa muda wa miaka mitatu kutokana na kutokuwepo kwa uwazi katika matumizi ya fedha na kukidhi vigezo vya utawala bora, TFF wamekuwa hawapati hizo fedha,” alisema Shonza. Shonza alisema kazi kubwa imefanyika kurekebisha dosari zilizokuwepo za kiuhasibu na utawala bora hivyo uwezekano ni mkubwa TFF na ZFA kuanza kupokea msaada huo wa fedha mapema mwaka huu.
4
WADAU wa kilimo cha alizeti mkoani Dodoma, wameiomba serikali kuandaa mafunzo maalumu kwa maofi sa ugani, hatua itakayowaongezea uwezo wataalamu hao katika kutoa elimu stahiki kwa wakulima wa zao hilo.Ombi hilo lilitolewa na wadau hao wakati wa kikao cha wajumbe wa Bodi ya Taasisi ya Kuendeleza Mifumo ya Masoko ya Kilimo Tanzania (AMDT), ambao walifanya ziara hivi karibuni mkoani Dodoma kwa lengo la kujifunza na kuona changamoto zinazowakabili wakulima wa zao hilo.Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wadau hao katika Wilaya za Bahi na Kongwa walisema, changamoto kubwa ambayo wakulima hao wanakabiliana nazo ni kukosekana kwa wataalamu wa kilimo waliobobea katika kilimo cha zao hilo.Walisema pamoja na changamoto hiyo, pia kuna idadi ndogo ya maofisa ugani ukilinganisha na mahitaji halisi ya idadi ya wakulima waliopo katika maeneo mengi mkoani humo.Mmoja wa wadau hao, Yohana Mwanjara ambaye anajihusisha na usambazaji wa mbegu na pembejeo kwa ajili ya alizeti alisema, licha ya jitihada kubwa ambayo serikali imekuwa ikifanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, bado tatizo la ukosefu wa wataalamu wenye weledi wa zao hilo ni kikwazo kikubwa. Alisema wengi wa wataalamu waliopo hawaendani na mabadiliko na teknolojia za kilimo zilizopo na hivyo kuwa kikwazo katika kumsaidia mkulima.“Unamkuta mkulima anahangaika kupata maarifa ya nini cha kufanya lakini hawezi pata msaada matokeo yake unakuta mkulima huyu anaishia kulima tu kwa mazoea,” alisema Mwanjala.Akiielezea changamoto hiyo, Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Kongwa, Jackson Shija alikili kuwepo kwa tatizo hilo na kuongeza kuwa mbali na changamoto ya elimu duni ya zao la alizeti kwa maofisa ugani, aliitaja changamoto nyingine kuwa ni uwepo wa idadi ndogo ya maofisa ugani kama kikwazo kingine katika kumfikia mkulima mmoja mmoja.“Idadi yetu ni ndogo ukilinganisha na idadi ya wakulima waliopo, hali hii imetulazimu wakati mwingine kuwatumia maofisa mifugo kusaidia kwenye maeneo ambapo hatuwezi kufika na hii kiukweli ni changamoto kubwa maana hata ambapo tunaweza fika wakati mwingine unakuta baadhi yetu uelewa wa zao hili kuwa ni mdogo na hata kuzidiwa maarifa na wakulima,” alisema Shija.Hadi sasa takribani maofisa kilimo 38 pekee ndio wanaotajwa kupata mafunzo maalumu kuhusu zao hilo ndani ya mkoa huo, idadi inayotajwa kuwa ni ndogo ukilinganisha na idadi ya wakulima takribani 33,400 waliopatiwa mafunzo rasmi ya zao hilo.Katika kuhakikisha mkoa wa Dodoma unaondokana na changamoto hiyo, na kulifanya zao hilo kama mojawapo ya mazao ya kibiashara yanayotegemewa na mkoa huo, uongozi wa Serikali mkoani humo umeanza mkakati wa kuwapatia mafunzo maalumu maofisa ugani ili kuwaongezea umahili katika kutoa elimu na huduma kwa wakulima.Hatua hiyo inatajwa kuwa itachochea katika kuongeza hamasa kwa wakulima wengi kujihusisha na kilimo cha zao hilo na hivyo kuvutia wawekezaji wengi kuwekeza viwanda vitakavyokuwa vikichakata mazao yatokanayo na zao hilo.
3
MATUMAINI ya Juventus katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya yako kwa Cristiano Ronaldo baada ya timu hiyo kuwa nyuma kwa mabao 2-0 dhidi ya Atletico Madrid wakati zikicheza mchezo wa pili wa hatua ya 16 utakaofanyika leo mjini Turin.Mbali na mchezo huo, pia kutakuwa na mechi zingine leo wakati mabingwa wa England, Manchester City watakapokuwa wenyeji wa Schalke 04 katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Etihad.Mechi za michuano hiyo zitaendelea tena kesho wakati Barcelona itakapocheza dhidi ya Olympique Lyonnais. “Kwa kweli hatukutarajia kabisa kufungwa 2-0 katika mchezo wa kwanza, lakini lolote linaweza kutokea katika mchezo wetu huo wa marudiano, na tunataka kufanya kweli mbele ya mashabiki wetu, “ alisema Ronaldo katika Tv ya Juventus kuhusu mchezo huo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Allianz.“Huu ni usiku wa aina yake, ni wa ajabu; ni usiku wa Ligi ya Mabingwa,” aliendelea kusema. “Timu iko vizuri na wachezaji wanajiamini kucheza mchezo mkubwa na mimi niko vizuri pia.Nimewaambia mashabiki, nafikiri mchezo utakuwa na matokeo chanya kwetu. “Jiandaeni kupindua matokeo!” Mabingwa hao watetezi ambao wametwaa ubingwa wa Italia mara saba walimnunua Ronaldo katika kipindi kilichopita cha majira ya joto akitokea Real Madrid kwa ada ya dola za Marekani milioni 117.Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 aliifungia Real Madrid bao la ajabu la mpira wa tiktaka huko Turin Aprili mwaka jana na kuitoa Juventus katika michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.Matarajio ni makubwa mchezaji huyo kufanya kile kama alichokifanya wakati akiibeba Real Madrid pale alipoifungia timu hiyo `hattrick’ dhidi ya Wolfsburg Aprili mwaka 2016 huku klabu hiyo ya Hispania ikiuanza mchezo ikiwa nyuma kwa mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza.Juventus mara nane imetoka nyuma katika mashindano hayo makubwa Ulaya na kushinda, ikiwemo mchezo wa robo fainali wa mwaka 1996 dhidi ya Real Madrid wakati ikielekea kutwaa taji hilo la Ligi ya Mabingwa. Pia timu hiyo ilitwaa taji hilo mwaka 1985, lakini walijikuta wakimaliza wa pili mara tano tangu walipotwaa taji hilo kwa mara ya mwisho, ikiwemo mara mbili katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
4
POLISI jijini Mwan- za imemuua mtu mmoja baada ya kuwa katika mapambano ya kurushiana risasi bai- na yake na watu wanao- daiwa kuwa majambazi.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro alisema shambulio hilo la aina yake limetokea Juni 3, mwaka huu 6.30 usiku katika eneo la Beijing Construction Engineering Group (BCEG) lililopo eneo la Uwanja wa Ndege katika Manispaa ya Ilemela.Alisema katika shambu- lio hilo, polisi wamekamata silaha aina ya shotgun iliyo- futwa namba zake halali za usajili ikiwa na risasi mbili na mapanga mawili kutoka kwa watu wanne wanaodai- wa kuwa ni majambazi.“Kwenye tukio hilo watu watatu walifanikiwa kuto- roka kusikojulikana na mtu mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 35-40 na ambaye hajafahamika alifariki katika mashambu- liano hayo yaliyohusisha askari wetu na majambazi,” alifafanua Kamanda Muliro.Alisema polisi walipata taarifa za kiintelejensia kwamba katika eneo hilo la BCEG, kuna majambazi wamevamia eneo hilo na ndipo polisi walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio na kuwakuta majambazi hao wanne na kuanza kurushiana risasi za moto.“Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hos- pitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure kwa utam- buzi na uchunguzi zaidi,” alisema na kuongeza kuwa Polisi inaendelea kuwasaka majambazi hao walioto- roka na watakapopatikana watachukuliwa hatua kali za kisheria.Kamanda Muliro am- etuma salamu kwa watu wanaojihusisha na matukio ya uhalifu waache mara moja kwa madai kuwa ni kinyume cha sheria na kwamba kikosi chake kitakuwa imara muda wote kudhibiti uhalifu wa aina zote.“Tunawaomba wananchi waendelee kutupa ushiriki- ano kwa kutupatia taarifa za uhalifu na wahalifu mapema ili tuweze kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyom- bo vya sheria,” aliongeza.Kamanda Muliro amewa- hakikishia wananchi kuwa Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kuhakikisha Waislamu wanasherehekea bila hofu na kwa amani na utulivu sikukuu ya Idd-el- Fitr.
3
MKOA wa Tabora unatekeleza mipango mbalimbali kuboresha kilimo ikiwemo kuwezesha upatikanaji wa matrekta ili kuinua pato la wakulima na mkoa kwa ujumla. Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri alilieleza gazeti hili kwamba mkoa huo utatumia fursa ya mradi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) wa kukopesha wakulima matrekta na kuhakikisha hakuna chama cha ushirika au mtu binafsi atakayetumia fursa hiyo kufanya udanganyifu au kujinufaisha. “Mkoa unausimamia mradi huu kupitia vyama vya ushirika. Vyama vya ushirika vinavyokusudiwa ni vyenye uchumi unaowezesha kukopeshwa. Vyama hivi visiwe na madeni. Lakini kwa watu binafsi kinachofanyika ni uhamasishaji na kuwa na uhakika nao na ofisi ya Mkuu wa Mkoa inatumika kama muandaaji,” alisema Mwanri. Alisema kila hatua inafuatiliwa kwa karibu kwani majina ya wanaoomba kupatiwa matrekta hayo yanayotolewa kwa njia ya mikopo au malipo ya fedha taslimu yametoka wilayani, kwenye kata na kwa watendaji walioko kwenye vijiji.Bei ya trekta ni kati ya Sh mil 38.2 na Sh mil 61.5. Naye Ofisa Kilimo wa Mkoa waTabora, Modest Kaijage alisema hadi sasa maombi ya mikopo kwa ajili ya matrekta hayo ni 105 na kwamba watu binafsi 43 wameshatanguliza fedha za awali Shilingi milioni mbili kila mmoja na kati ya hao,saba wameshapokea matrekta. Alitaka mafunzo yatolewe kuhusu matumizi ya matrekta hayo. Akizungumzia mradi huo, Meneja wa NDC, Said Tunda, alisema matrekta 72 ni kwa ajili ya watu binafsi na 55 kwa ajili ya vyama vya ushirika vilivyoko chini ya chama kikuu cha ushirika cha mkoa, Igembesambo na kwamba yana teknolojia ya kisasa.
3
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Rage alisema ameambiwa fedha hizo tayari zimeshatumwa kwa klabu hiyo, hivyo ni jukumu la uongozi kuhakikisha masuala ya kimaendeleo yanapatikana.Alisema dola za Marekani 300,000 (zaidi ya Sh milioni 600 za Tanzania) ambazo Simba imepewa kwa kumuuza Okwi ni nyingi kama zikitumika vizuri na kwamba kama zikitumiwa vibaya si fedha nyingi.Pia Rage amesema Simba imepewa dola za Marekani 19,000 (karibu Sh milioni 40) kama riba kutokana na kuchelewa kupewa fedha karibu miaka mitatu sasa na kushauri viongozi wahakikishe wanazitumia vizuri na si kuelekeza katika malipo ya madeni.“Klabu ina changamoto nyingi za kufanya, sitaki kusema wafanye kitu gani, lakini Simba ina mambo mengi ya maendeleo waelekeze huko, hata kujenga sehemu ambapo wachezaji watakuwa wanaweka kambi yao ” alisema Rage na kuongeza kuwa anashukuru kusikia fedha hizo zimepatikana kwani wapo baadhi ya watu walikuwa wakimshutumu kwamba amekula fedha hizo. “Nilipigania sana hizo fedha wengine wakawa wananishutumu. Naamini sasa kile nilichokuwa nakifanya kimepatikana na nataka kiinufaishe Simba na si kuambiwa zimelipia madeni ya klabu,” alisema.Akizungumzia suala hilo, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, alisema atalizungumzia wakati wowote kuanzia leo.“Nitaitisha mkutano na waandishi katika siku mbili hizi, nitafafanua mambo mengi,” alisema Manara.Okwi aliuzwa kwa dola za Kimarekani 300,000 Etoile du Sahel ya Tunisia miaka mitatu iliyopita, ambapo Etoile haikulipa fedha hizo Simba na baadaye ikaingia kwenye mgogoro na Okwi, aliyedai hakulipwa mshahara wake kwa miezi mitatu.Okwi akawafungulia Etoile kesi Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) na akaomba wakati mgogoro wao unaendelea, aruhusiwe kuchezea timu yoyote kulinda kipaji chake. Hivi sasa Okwi anacheza soka nchini Denmark.
4
CHUO Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIUT) kimesema kimefanya mabadiliko makubwa ili kuondoa upungufu uliokuwa ukikikabili ikiwemo katika safu ya uongozi na kutokuwepo kwa Baraza la Chuo, hivyo kushindwa kudahili wanafunzi wapya katika mwaka wa masomo 2017/18.KIUT imekiri kuwa changamoto hizo pamoja na kwamba zimekitikisa na kuathiri utendaji kazi, lakini zimewajenga na kuwaimarisha kimuundo na kitaasisi, huku wakiahidi kuendelea kuwa na mawasiliano na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).Aidha, kimesema kinatarajia kupeleka maombi TCU kuwaomba kuruhusiwa kudahili wanafunzi kwenye shahada za uzamili na uzamivu, ili kuwaongezea wanafunzi weledi, ujuzi katika fani mbalimbali. Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Jamidu Katima alisema hayo jijini Dar es Salaam katika mahafali ya kwanza ya KIUT, ambayo jumla ya wahitimu 753 walipatiwa shahada mbalimbali.Kuhusu upungufu, Profesa Katima alisema katika mwaka wa masomo 2017/18, KIUT ilishindwa kudahili wanafunzi wapya kutokana na kukabiliwa na upungufu kadha wa kadha ikiwamo kutokuwa na namba ya wanataaluma wa kudumu inayokidhi idadi ya wanafunzi waliokuwepo. Alizitaja upungufu wa wafanyakazi wenye sifa stahiki zinazokidhi viwango vinavyokubalika na mwongozo wa ubora wa elimu wa TCU, kuwepo wafanyakazi wa kigeni wasiokuwa na vibali stahiki vya kufanya kazi nchini.“Ninafurahi kueleza kua kuanzia mwezi wa tatu chuo kimefanya mabadiliko makubwa ili kuondosha mapungufu hayo na katikakufanya maboresho hayo chuo kimeendelea kuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na Tume ya Vyuo Vikuu,” alisema Profesa Katima.Profesa Katima alisema ni wazi kua changamoto hizo zilitikisa na kuathiri utendaji wa kazi wa chuo, lakini kwa upande mwingine zimewajenga na kuaimarisha kimuundo na kitaasisi. Alisema kwa sasa chuo kina jumla ya wafanyakazi 269, jumla ya wafanyakazi wanataaluma ni 138 wakijumuisha maprofesa 11 na wanataaluma wenye shahada za uzamivu 20.Kuhusu wahitimu, alisema chuo kinawatakia mafanikio mema katika shughuli watakazokwenda kuzifanya kwa ajili ya ujenzi wa Taifa na kuwaasa kuwa tayari kukabiliana na changamoto za maisha ambazo ni nyingi.“Kwa kuanzia inawezekana kabisa kati yenu kuwa watakaokaa muda mrefu bila kupata ajira hili ni jambo la kawaida sana na isiwasababishie kukata tamaa ya maisha na kujikuta mnadumbukia katika mambo ambayo yatwaondoa katika mstari a matumaini,” alisema. Aliwasihi kuwa tayari kujitolea kwa ujira mdogo au bila ujira kabisa ili kupata uzoefu wa kazi na kuepuka kupata muda wa kushawishika kufanya mambo yasiyostahili, na kati yao watakaopata ajira vijijini wasichague maeneo ya kufanyia kazi bali jambo la msingi kuhakikisha elimu waliyoipata inawasaidia kutatua matatizo ya Watanzania.
3
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, ameipongeza Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la JAMAFEST 2019, ambalo kwa mwaka huu limepangwa kufanyika Tanzania. Tamasha hilo linalozihusisha nchi za Afrika Mashariki na Kati hufanyika kila baada ya miaka miwili katika moja ya nchi zilizomo kwenye umoja huo wa EAC kwa kushirikisha michezo mbalimbali ya kijadi ikiwemo ngoma za asili, bao, rede, vyakula vya asili na michezo mingine.Akizungumza kwenye kikao hicho cha pili cha maandalizi ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Dar es Salaam kuanzia Septemba 21 hadi 28, Waziri Mwakyembe, alisema ameridhishwa kwa mipango mkakati iliyoandaliwa kwa ajili ya tamasha hilo kubwa, lakini kazi kubwa iliyopo mbele yao kama wizara ni kusaka fedha zitakazofanikisha kufanyika kwa tamasha hilo.“Naipongeza kamati ya maandalizi kutokana na mipango mizuri waliyoiandaa kwa ajili ya tamasha kubwa lililopo mbele yetu, kitu cha msingi sasa tunachotakiwa ni kusaka fedha ambazo ni sh Bilioni 2.9, ili kufanikisha tamasha hilo ambalo kama wenyeji nataka liwe kubwa na mfano kuliko ilivyokuwa kwenye mataifa yaliyopita,” alisema Mwakyembe.Alisema, kiasi hicho cha fedha zinazohitajika kufanikisha mashindano hayo ni kikubwa hivyo ameziomba kampuni mbalimbali nchini kujitokeza kuchangia na wao kutangaza bidhaa zao ili kufanikisha tamasha hilo ambalo limevuta hisia za watu mbalimbali kutoka kila pembe yadunia.Aidha Mwakyembe, amevitaka vikundi mbalimbali vya ngoma za asili muziki wa Bongo Fleva, na michezo mingine ya asili kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi ya kutosha ili kufanya vizuri na kubeba ushindi wa jumla katika tamasha hilo linalofanyika nchini kwa mara ya kwanza.Pia Waziri Mwakyembe alisema amepanga kukutana na baadhi ya wasanii wanaofanya vizuri kwenye muziki wa Bongo Fleva akiwemo Nasib Abdul ‘Diamond’, Ali Kiba, Ruby, Nandy, Saida Karoli na Rayvany ili kuwaomba washiriki walau kwa siku moja ili kunogesha tamasha hilo na kuwavutia watu mbalimbali kuhudhuria na kujionea utamaduni wa mataifa mbalimbali ya Afrika Mashariki.“Nimepanga kukutana na vijana wangu hawa wa Bongo Fleva, niwaombe watoe mchango wao hata kwa siku moja kuimba bure kuchangia kwani kitendo cha wao kukubali ni faida kubwa kwani wataonekana na kujitangaza ulimwengu mzima na kupandisha thamani ya muziki wao,” alisema Maziri Mwakyembe.Kiongozi huyo pia aliwapongeza wajumbe kutoka Zanzibar, kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano huo wa pili wa maandalizi na kusema kwamba huo ndio unaonyesha uhalisia halisi wa Muungano.
4
MFANYABIASHARA Rostam Aziz, Kampuni ya GSM, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete wameichangia Yanga zaidi ya Sh milioni 500 katika hafl a iliyofanyika Dar es Salaam jana.Katika hafla hiyo iliyofanyika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam na Waziri Mkuu Majaliwa akiwa mgeni rasmi, GSM iliahidi kuchangia Yanga Sh milioni 300 huku Rostam akichanga Sh milioni 200, Majaliwa akichangia Sh milioni 10 na Kikwete milioni tano.Harambee hiyo iliendelea hata baada ya kuondoka kwa Waziri Mkuu na baadae Kikwete, ambapo wanachama waliendelea kutoa fedha na ahadi ili kuisaidia Yanga kufanya usajili wa nguvu pamoja na uendeshaji wa klabu hiyo.Akizungumza kabla ya kuchangia, mgeni rasmi huyo aliwapongeza Yanga kwa kuwa watulivu kipindi ambacho walikuwa wakikabiliwa na changamoto ya kifedha, lakini timu yao ilifanya vizuri kwa kumaliza ligi katika nafasi ya pili na kupata ushiriki ujao kimataifa.“Timu ya mpira ili iweze kufanya vizuri ni lazima iwe na fedha kwa ajili ya uendeshaji kuwalipa makocha na wachezaji, bila Yanga imara hatuwezi kuwa na Simba imara, kila mmoja achangie kuiwezesha timu kuwa na uchumi mzuri,” alisema.Aliupongeza uongozi mpya akisema umeanza kuonesha mwanga wa mafanikio mbele akiwahimiza watengeneze mfumo utakaosaidia kuongeza mapato ya ndani. Pia, akimpongeza Kocha Mwinyi Zahera kwa kufanya vizuri msimu uliopita.Kwa upande wake mgeni maalumu wa tukio hilo , Kikwete alisema kuna haja kwa klabu za Tanzania ku- fanya uwekezaji kwa vijana ili kupata wachezaji bora watakaosaidia timu ya taifa baadaye. Kikwete alisema klabu zinatumia pesa nyingi kuleta makocha kwa ajili ya kufundisha wachezaji wa nje huku watu wakibaki kuwasifia lakini kwenye timu ya taifa hawamo na kusisitiza kuwa wasipoweka juhudi kwenye timu za watoto watabakï kuwa mafahali wa wengine.Aliwataka Yanga kuten- geneza mfumo mzuri wa uendeshaji, kuwa wa kisasa na kuwekeza kwenye timu za watoto. Pia, alihimiza viongozi wapya wa Yanga kurudisha hamasa kwa mashabiki kama iliyokuwa zamani. “Mnabaki kuwasifia akina Kagere (Meddie) waki- ondoka hatuwaoni kwenye timu za taifa. Ifike mahali muone fahari kwa wachezaji wa ndani na kuwaendeleza wale wenye vipaji, “alisema.Aliwahimiza Yanga kutengeneza mfumo endelevu utakaosaidia kuongeza mapato ya ndani badala ya kuwategemea wafadhili na mwisho wa siku wakipata matatizo na klabu inateter- eka. Pamoja na hayo, alimpongeza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kushiriki tukio hilo bila kujali ushabiki wake akisema huo ndio uongozi bora na kuongeza kuwa kama mtu akiwa kiongozi haipendezi kutumia ushiriki wake wa kimpira kukandamiza klabu nyingine.Mbali na michango hiyo pia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliwapatia Yanga eneo Kigamboni kwa ajili ya kujenga uwanja wa soka. Katika hatua nyingine, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakale- bela aliwatambulisha wachezaji wapya wawili, Abdulaziz Makame na mfungaji bora wa Uganda Juma Balinya aliyejiunga nao kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Polisi FC ya Uganda.
4
Na Mwandishi Wetu-Morogoro UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi  (UVCCM), umesema Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, hafahamu wala hajui dhana ya demokrasia ya vyama vingi,  jambo linalomfanya kiongozi huyo kila siku kuilaumu Serikali. Kauli hiyo ya UVCCM, imekuja siku chache baada ya Sumaye kudai kwamba watawala wa Serikali wa sasa wanaiogopa Katiba Mpya na kugeuka kuwaandama wapinzani kwenye mfumo wa vyama vingi. Hayo yalisemwa jana mjini hapa na Kaimu  Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, alipokuwa akizungumza na vijana wa CCM Mvomero wakati akielekea mkoani Dodoma ambapo alisema hatua hiyo ya Sumaye ya kudai kuna mfumo mgumu wa demokrasia haileti mantiki kwa sasa. Alisema msingi wa kuruhusiwa vyama vingi nchini si kukwamisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii au kuwafanya wananchi kila siku wakusanyike viwanjani kusikiliza mikutano ya hadhara bila kutilia maanani uzalishaji mali viwandani, mashambani na maofisini. “Vijana wenzangu hata ligi ya soka au mashindano ya kutafuta warembo yana msimu na vipindi vyake, timu haziwezi kushiriki michuamo mwaka mzima bila wachezaji na waamuzi kupumzika, domokrasia ya wapi ambayo haina vipindi vya kampeni. “…uchaguzi au watu kutakiwa kufanya kazi za maendeleo acheni kusikiliza poroja za wanasiasa waliochoka vijana chapeni kazi sasa ili kujiletea maendeleo endelevu,” alisema Shaka . Alisema UVCCM imeshangazwa na matamshi ya Sumaye anayedai kuwa serikali ya awamu ya tano inakandamiza  misingi ya demokrasia kwasababu tu imevitaka vyama kuendesha shughuli za kisiasa kwenye mikutano ya ndani ili kuwapa nafasi wananchi kujituma na kuzalisha. Kaimu huyo Katibu Mkuu alisema hata kanuni na fomula za masomo ya hesabu, kemia na baiolojia hazilingani katika kupata majawabu halisia hivyo akataka ifahamike  demokrasia nayo ina vipindi vya kampeni , mikutano ya hadhara, uandikishaji, upiga kura, kuhesabu na kutangazwa matokeo . “UVCCM tunamfahamu Sumaye toka akiwa Naibu Waziri wa Kilimo hadi Waziri Mkuu, hana rekodi nzuri ya kiutendaji ilioleta tija, mafanikio au ufanisi katika maeneo  aliyoyaongoza, yaonyesha ni mshabiki wa hadithi kuliko kufanya kazi,” alisema. Kutokana na hali hiyo alimtaka mwanasiasa huyo kufuta ndoto na fikra siku moja itatokea CCM kudondoka madarakani kisha yeye au mshirika wake Edward Lowassa mmoja kati yao awe urais wa Tanzania. “Tanzania imechoka kuwa ombaomba wa kila msaada toka kwa wahisani na washirika wa maendeleo, Serikali ya CCM  imezinduma usingizini na kujitambua, haitaruhusu upuuzi usio na manufaa ili ionekane demokrasaa maana yake ni mikutano ya hadhara bila uzalishaji mali,” alisema
3
Na GABRIEL MUSHI, DODOMA WATANZANIA 25, wamekamatwa nje ya nchi kwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya mwaka 2015. Kauli hiyo imetolewa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Anthony Mavunde, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2015. Kwa mujibu wa Mavunde, Watanzania hao walikamatwa katika nchi za China (13), Brazil (9) na Zambia (3) ingawa hadi sasa hakuna aliyenyongwa kwa tuhuma hizo. “Taarifa imebainisha kuwa mwaka 2015 biashara ya dawa za kulevya iliendelea kufanyika kwa kiwango kikubwa, huku nchi ikishuhudia kuibuka tena kwa biashara ya mandrax baada ya kukamatwa kwa kilo 5.1 za dawa hizo mkoani Dodoma na Ruvuma. Dawa za aina hiyo zilikamatwa kwa mara ya mwisho mwaka 2010. “Wanaume wameendelea kuwa wahusika wakuu wa biashara hii, ingawa takwimu zinaonyesha pia wanawake nao wanajihusisha na biashara hiyo kwani kati ya watu 15,815 waliokamatwa nchini kwa tuhuma hizo, wanawake walikuwa 1,436. “Idadi hii ni kubwa hasa ikizingatiwa wanawake kiutamaduni ni watu wanaoaminika kwa kutokuwa na kawaida ya kujihusisha na vitendo vya uhalifu,” alisema Mavunde. Pamoja na hayo, alisema matumizi ya bangi nchini yameshuka ingawa biashara hiyo imeendelea kushika kasi.
3
NAIROBI, KENYA RAIS Uhuru Kenyatta ameunda mahakama maalumu kuchunguza mienendo ya Jaji wa Mahakama ya Juu zaidi, Jackton Ojwang. Katika taarifa yake maalumu iliyotolewa juzi, Uhuru alisema kuwa kuondolewa kwa jaji huyo kutategemea matokeo ya uchunguzi huo wa mahakama. Jopo la mahakama hiyo linaongozwa na mwenyekiti Jaji Alnashir Visram na wajumbe wakiwa majaji wastaafu, Festus Azangalala, Ambrose Weda, Andrew Bahati Mwamuye, Lucy Kambuni, Sylvia Wanjiku Muchiri na Amina Abdalla. Uhuru alisema mienendo ya Jaji Ojwang inapaswa kuchunguzwa kutokana na maswali mengi yanayoulizwa juu yake. Alisema hatua ya kuundwa kwa mahakama hiyo dhidi ya Ojwang, imetokana na ombi lililotolewa na Tume ya Huduma za Mahakama ya Kenya (CSJ). Ombi hilo liliwasilishwa na kamati ya CSJ chini ya uenyekiti wa Nelson Oduor Onyango na wajumbe wengine wanane. “Katika utekelezaji wa kazi zake, mahakama itaandaa na kuwasilisha ripoti na mapendekezo kwangu na baada ya hapo nitachukua uamuzi kulingana na mamlaka niliyopewa na sheria,” alisema Rais Uhuru.  Katika ripoti iliyowasilishwa kwa Rais, Ojwang anashutumiwa kuwa na mienendo isiyofaa, kuibua migogoro isiyoendana na miiko ya kazi yake na ukiukaji wa kanuni za kazi yake. Ojwang anaelezwa alikuwa mmoja wa majaji wa Mahakama ya Juu zaidi walioendesha kesi katika Kaunti ya Migori ilhali ikifahamika ni mshirika wa karibu wa Gavana wa kaunti hiyo, Okoth Obado. Wajumbe tisa wa CSJ walisema Obado aliweka lami kwenye barabara inayoelekea makazi binafsi ya kijijini ya Jaji Ojwang, kitu kinachotia shaka. Kwa maoni yao, Ojwang angepaswa kuifahamisha mahakama na wadau wote juu ya ushirika wake wa karibu, kwa maana ya masilahi aliyonayo kwa gavana huyo, lakini hakufanya hivyo hadi alipopingwa.  “Kutokana na tuhuma zilizomkabili Jaji Ojwang, tume ya JSC ilichunguza kwa makini kwa marefu na mapana na kubaini kuwa kuna sababu za kutosha za kumwomba Rais kuunda mahakama ya kumwondoa madarakani, na kuidhinisha ombi kulingana na sheria,” alisema Jaji Mkuu wa Mahakama ya Juu, David Maraga.  Aidha Rais Uhuru amewateua wanasheria Paul Nyamodi na Stella Munyi kuwa washauri wa  kusaidia mahakama hiyo maalumu kwa uchunguzi wa Ojwang.  Alisema Peter Kariuki na Josiah Musili watahudumu pamoja kama makatibu wa mahakama hiyo maalumu.
2
WAKATI binti wa miaka 17 aliyekuwa akifanya kazi za ndani jijini Dar es Salaam akieleza ukatili aliokuwa akifanyiwa na bosi wake, ikiwemo kuwekewa mwiko sehemu za siri hali inayosababisha asione siku zake (hedhi) kwa mwaka mmoja sasa, taasisi mbalimbali zimeelezwa kushangazwa na ukatili wa aina hiyo na kutaka hatua kali zichukuliwe.Mkuu wa Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Vumilia Nyamoga alilaani ukatili huo uliofanywa na mwajiri wa mtoto huyo, Happines Mathew ambaye ni muuguzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na kutaka vyombo vya dola kuchukua hatua katika suala hilo.DC Nyamoga alisema Happiness na mumewe, Dk Tito Lunobo, ni wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na wanawajibika katika suala hilo la ukatili dhidi ya binti huyo. “Ninalaani ukatili wa kijinsia uliofanywa kwa binti huyo ambaye nimemuona kwa macho yangu, ni tukio la kusikitisha sana lazima tulisemee hili tusikae kimya.Unyama aliofanyiwa huyu binti unashangaza na hauingii akilini kama unaweza kufanywa na watumishi wa afya, unawezaje kumwadhibu mtoto wa mwenzio kwa kumuingiza mwiko kama fundisho la kumuonesha uchungu wa kuzaa kwa kosa la kumdondosha mtoto?” Alihoji Nyamoga.“Navitaka vyombo vya dola vichukue hatua kali kwa wote pamoja na watendaji wote ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa wakipotosha ukweli kwa kumkandamiza binti ambaye alipata mateso kwa muda wa miaka mitatu mfululizo.” Pia mkuu huyo wa wilaya alisema Ofisi ya Ustawi wa Jamii na Polisi (Chamwino na Temeke) wanapaswa kufuatilia na kuangalia upya jalada la kesi ya binti huyo, ilikuwaje lilifungwa na mambo yakaishia nyumbani wakati binti huyo amefanyiwa ukatili ambao ni jinai. Alisema ofisi yake itahakikisha inasimamia haki ya binti huyo ilipokwama na kuhakikisha kuwa binti huyo anafanyiwa vipimo na kupata tiba sahihi.DC Nyamoga alisema anamshukuru hata msamaria mwema aliyetoa habari za kikao cha ukoo kutoa fidia ya Sh milioni 1.3 na huo ni ushahidi kuwa kuna uovu ulikuwa unafichwa.Kauli ya HappinessAkizungumza kwa njia ya simu, Happiness alisema suala liko Polisi, hivyo hawezi kusema kitu na kama kuna jambo lolote waulizwe Polisi.Diwani azungumzaDiwani wa Kata ya Manchali, Mary Mazengo alisema alikwenda kumuona binti huyo na alichokiona ni ukatili ambao unaumiza moyo. “Binti ana majeraha ya kupigwa na mwiko kichwani, nimehesabu ana majeraha 19 na sehemu zake za siri zimeharibika vibaya,” alisema Mazengo na kuongeza kuwa pia binti huyo ana makovu ya kuchomwa na pasi mgongoni, macho na midomo yake, na matatizo ya kiafya.Alisema mara ya kwanza binti huyo alipelekwa hospitali na mama wa mtuhumiwa, lakini kinachoonekana madaktari wa Dar es Salaam na Dodoma wana mawasiliano na huyo binti alipimwa kutokana na maelekezo. Alisema wanataka kutafuta utaratibu ili binti atibiwe na madaktari watakaowachagua wao (halmashauri) na si madaktari wanaopata maelekezo ya familia kwani huyo binti hatapata matibabu kikamilifu.Binti mwenyewe anasemaje?Akisimulia mkasa huo, binti huyo alisema sasa analazimika kuvaa kofia muda wote ili kuficha makovu ya kichwani yaliyotokana kupigwa na mwiko kila mara.Katika mazungumzo hayo, binti huyu alidai pia macho yake yamekuwa mekundu kwa kile alichodai kusuguliwa macho mara kwa mara na mwajiri wake. Anasema kwa sasa ana uoni hafifu. Alisema alimaliza darasa la saba katika Shule ya Msingi Manchali mwaka 2016, hakufaulu ndipo alipochukuliwa na ndugu yake, mtoto wa mama yake mkubwa, Happiness Mathew au Happiness Job ambaye ni Muuguzi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili akafanye kazi za ndani. Alisema katika maisha yake alikuwa akikutana na vipigo vya mara kwa mara kwani mwajiri wake huyo hata akimkuta mtoto analia alikuwa anamwangushia kipigo.Alisema kuna siku mtoto alikuwa akicheza na akaanguka, dada huyo aliporudi akamsema hamuangalii mtoto kwa vile hajui uchungu wa kuzaa na atamfanyia kitu ili asikie uchungu kama huo. Ndipo alipompiga na kuchukua mwiko ambao aliuingiza sehemu za siri na tangu wakati huo ni zaidi ya mwaka sasa hajapata siku zake (hedhi) na amekuwa akipata maumivu anapoenda haja ndogo. Binti huyo anasema pia aliwahi kupewa adhabu ya kulala wima mpaka asubuhi. “Siku hiyo alikasirika akasema utalala ukiwa umesimama, muda wa kulala ulipofika akaniingiza chumbani kwake, akaniambia adhabu yako utasimama hadi asubuhi, basi yeye akalala kitandani mimi kwa hofu nikabaki nimesimama mpaka asubuhi,” alidai.Binti huyo alisema alikuwa akilipwa Sh 50,000 mshahara wa mwezi na fedha hizo alikuwa akitumiwa mama yake mzazi moja kwa moja. Akimbilia polisi “Kuna siku nikajiuliza nitateseka mpaka lini, pale nyumbani aliletwa mfanyakazi mwingine wa ndani, tukapanga tutoroke, lakini nikaamua kwenda hadi Kituo cha Polisi Chang’ombe nikatoa maelezo yangu na mhusika alikamatwa,” alisema. Alisema baada ya mwajiri wake kukamatwa aliwekwa rumande na yeye kutoa maelezo yake na kisha alikwenda kukaa nyumbani kwa mjumbe wa mtaa.Wakata tamaaAlisema isingekuwa rahisi kwao kuendelea na kesi jijini Dar es Salaam kwani hawakuwa na sehemu hata ya kulala. “Tuliamua kesi iishe tu hatuna mtu wa kutusaidia, isitoshe hatukuwa hata na pa kukaa kufuatilia kesi hiyo mpaka iishe, mama aliamua tu turudi nyumbani,” alisema. Alisema waliporudi Dodoma, ujumbe ulifika nyumbani kwao kuja kuomba msamaha. “Mama yake na Happiness alitumwa ili aje kumuombea mtoto wake msamaha ili mambo hayo yaishe na siku ya Jumanne iliyopita nilipelekwa hospitali kwa ajili ya kufanyiwa X-ray,” alisema.Hata hivyo, haelewi majibu ya vipimo hivyo kwani aliyempeleka alisema hakuonekana na tatizo wakati yeye anaumwa.Maumivu yapo wapi?Anasema hajatibiwa macho kwani hospitali waliyokwenda hakuna daktari wa macho na macho yamekuwa yakimsumbua na hata midomo yake imekuwa imevimba muda wote. Pia alisema amekuwa akipata maumivu ya kichwa kutokana na ukweli kuwa kuna wakati alikuwa akipigizwa ukutani mara kwa mara na maumivu ya shingo kutokana kukabwa mara kwa mara. Alisema anachohitaji sasa ni kusaidiwa ili apate matibabu kwani amekuwa na maumivu makali ya mwili na hajui atapata hedhi lini na hajui kilichovurugwa mwilini mwake hadi anakosa hedhi.“Sijui ule mwiko alioniingiza umeleta madhara gani katika mwili wangu naona nisaidiwe ili nifanyiwe vipimo,” alisema. Alisema alivunja ungo mwaka 2014 na alikuwa akipata hedhi kawaida, lakini baada ya kuingiziwa mwiko haoni kabisa hedhi.Mama mzazi asimuliaMama mzazi wa binti huyo, Rehema Richard alisema mwaka 2017, Happiness alikwenda kumuomba mtoto wake akamsaidie kazi za ndani na aliahidi atakaa naye vizuri. “Kumbe mtoto alikuwa akiteseka na alikuwa hataki nijue mtoto alikuwa akiteseka kwa kiwango hiki,” alisema na kuongeza alijua hayo alipoitwa katika shauri jijini Dar es Salaam.“Nilienda nikakuta mtoto kapigwa hata sura yake imebadilika, nikasema sina la kusema nipeni mwanangu nirudi naye nyumbani,” alieleza mama huyo. Alisema ingawa mama wa Happiness alimchukua binti huyo na kumpeleka hospitali, alipewa tu vidonge vya maumivu, “huyu anahitaji vipimo ili matatizo yake ya mwili yajulikane na yatibiwe.”Milioni 1.3/- kama fidiaMama wa binti huyu alisema baada ya kurudi na bintiye, kuliitishwa kikao cha ukoo iliamriwa suala hilo limalizwe kimila na familia ya Happiness iliagizwa kulipa fidia na yeye mwenyewe kukubali kutoa Sh milioni 1.3 kama fidia.“Januari 22, walitukabidhi hela hizo, nimeziweka tu,” alisema mama mzazi wa binti huyo. Nakala ya barua ya makabidhiano hayo ambayo gazeti hili inalo inaonesha fedha hizo zililipwa Januari 22, mwaka huu. Naye mama yake Happiness, Evelina Mchiwa ambaye pia ni mkazi wa Kijiji cha Manchali, alisema baada ya kupewa taarifa kuhusu kukamatwa kwa mwanawe alifika Dar es Salaam, na kumkuta akishikiliwa katika Kituo cha Polisi Chang’ombe. “Wakaandika jalada niliona suala hili tukalijadili nyumbani japo polisi walikuwa wakitaka suala hilo liende mahakamani,” alisema.Kwa upande wake kuhusu suala hilo la kuendesha kesi katika mahakama za Dar es Salaam, mama wa binti aliyefanyiwa ukatili alisema hakuwa na uwezo wa kuendesha shauri hilo akiwa Dar es Salaam, hakuwa na ndugu wala uwezo ndio maana aliamua kurudi nyumbani. Suala la binti huyo kufanyiwa ukatili liliibuliwa na msamaria mmoja ambaye alipiga simu kwa Ofisa Maendeleo wa Wilaya ya Chamwino, Sophia Swai aliyesema kwamba kuna binti ameletwa kutoka Dar es Salaam anaumwa baada ya kufanyiwa ukatili.Ilijulikana vipi?Sophia alisema kutokana na hamasa kwa wananchi kutoa taarifa juu ya matukio ya ukatili, suala hilo lilibuliwa na msamaria aliyempigia simu juu ya kuwapo kwa binti mwenye afya mbaya aliyefanyiwa ukatili jijini Dar es Salaam na kuamua kufuatilia tukio hilo kubaini ukweli wake. Swai alisema baada ya kupata taarifa hizo alikwenda kuonana na Mkuu wa Kituo cha Polisi Chamwino ambaye alifanya mawasiliano na OCD wa Chang’ombe, ambako ilibainika kuwa faili hilo limefungwa, jambo ambalo lilizua maswali kutokana na hali ya binti kuwa mbaya.Kamanda Temeke azungumzaAkizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Awadhi Haji alisema kadhia hiyo ya ukatili ipo katika Dawati la Jinsia na wanasubiri hati ya matibabu (PF3) ili kuifikisha mahakamani na haki itendeke.Alisema binti huyo ambaye anaonekana ana undugu na mtuhumiwa, alifika polisi Januari 4, mwaka huu kulalamikia ukatili anaofanyiwa. Kamanda Haji alisema baada ya kumsikiliza mlalamikaji, Polisi walishughulikia malalamiko hayo kwa kufanya upelelezi pamoja na kumkamata mtuhumiwa Happiness Job kwa mahojiano. Alisema baada ya kukamilika kwa upelelezi, shauri hilo halijaenda mahakamani kwa kuwa mlalamikaji ambaye ndiye shahidi wa kwanza katika shauri hilo, hajarejesha PF 3 kama inavyotakiwa.“Shauri hilo ni kama linakosa ushirikiano, mlalamikaji hajarejesha PF 3 ili twende mahakamani. Nimemwagiza Mkuu wa Upelelezi kuhakikisha kwamba wanalipeleka shauri hili mahakamani kwani suala kama hili halimalizwi kienyeji, kuna ukatili mkubwa hapa,” alisema Kamanda Haji. Kwa mujibu wake, katika mahojiano wakati wa upelelezi, familia hizo zilionekana kutaka suala hilo liishie kienyeji, wao wanataka mlalamikaji huyo kupata haki zake pamoja na waajiri wanaofanyia ukatili wafanyakazi wao kutambua serikali ina mkono mrefu katika kulinda wananchi wake. Alisema jamii inapaswa kukemea vitendo vya kikatili na kuviripoti mara moja Polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe.
3
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar inatarajia kupata Dola za Marekani milioni 150 kutoka Benki ya Dunia zitakazotumika katika kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya kukuza utalii na kustawisha miji katika visiwa hivyo.Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Khamis Omar alisema Washington kuwa Benki ya Dunia imekuwa mshirika mzuri wa maendeleo ya Serikali ya Zanzibar kutokana na misaada mbalimbali wanayoitoa katika kutekeleza miradi yao ya maendeleo.Omar alisema benki hiyo imesaidia kufadhili ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ya barabara zinazoingia mijini, Uwanja wa Ndege wa Zanzibar pamoja na bandari. Aidha benki hiyo pia imesaidia zaidi katika ujenzi wa uwanja wa ndege, kwa kujenga sehemu ya maegesho ya ndege, njia ya kutua na kurukia ndege na njia ambazo ndege zinapita kabla ya kuingia kwenye sehemu ya kurukia (runway).“Pia benki hii imekuwa ikisaidia miradi mbalimbali ya elimu Visiwani Zanzibar ukiwemo mradi wa kukuza matokeo na kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika shule za Zanzibar,” alisema Omar na kueleza kuwa hivi sasa wanatekeleza mradi mkubwa wa ustawishaji wa huduma za mijini ambao unafadhaliwa na Benki ya Dunia na mradi huo utasaidia kuboresha huduma muhimu katika Miji ya Zanzabar ikiwa ni pamoja na kuongeza vivutio vya utalii.
3
Na MWANDISHI WETU-ZANZIBAR BENKI ya makabwela (NMB) imetoa msaada wa kompyuta 50 kwa shule za msingi na sekondari za visiwani Zanzibar. Msaada huo ulikabidhiwa na Mkurugenzi wa NMB, Ineke Bussemaker kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Riziki Pembe Juma, aliyesema unalenga kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha elimu. Bussemaker alisema NMB inaunga mkono juhudi za Serikali za kukuza kiwango cha elimu nchini, hususan katika masomo ya Tehama. Alisema msaada huo utazinufaisha shule za msingi na sekondari tisa pamoja na chuo cha ualimu kimoja kitakachopatiwa kompyuta mpakato tano. “Kompyuta hizo ni sehemu ya kompyuta zaidi ya 250 ambazo tayari zimeshakabidhiwa Tanzania Bara kwa ajili ya shule za msingi na sekondari. Kompyuta hizo zilishatumika na benki ya NMB kwa miaka mitatu, huku zikiwa bado kwenye hali nzuri kwa ajili ya matumizi.  “Tumetoa msaada wa kompyuta 50 zilizokwishatumika miaka mitatu kwa ajili ya shule za msingi na sekodari, zipo katika hali nzuri kwa matumizi ya wanafunzi na wataalamu wetu wa ICT wamethibitisha na tunaamini zitatumika vizuri na kuwa na faida katika masomo ya Tehama,” alisema Bussemaker. Akipokea kompyuta hizo, Waziri Juma alisema msaada huo umetolewa wakati muafaka  kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
3
Na LEONARD MANG’OHA-DAR ES SALAAM KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeitaka Serikali kurekebisha sheria ya kanuni ya adhabu na ya ugaidi inayotoa adhabu ya kifo kwa makosa ya mauaji, uhaini na ugaidi. Pia kituo hicho kimempongeza Rais John Magufuli kwa kueleza bayana kwamba hatatekeleza adhabu ya kifo. Septemba 12 mwaka huu, wakati akimwapisha Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma, Rais Magufuli alisema hana mpango wa kunyonga watu hivyo asipelekewe orodha ya waliohukumiwa adhabu hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga, alisema adhabu ya kifo inakiuka haki ya msingi ya binadamu kuishi na kuondoa uwezekano wa mkosaji kujirekebisha, na badala yake inaendeleza ukatili dhidi ya ubinadamu. LHRC imezitaka mamlaka husika kuweka adhabu mbadala wa kifungo cha maisha  ili kuthamini uhai ambao ni haki ya kila binadamu. Aliitaka Serikali kutekeleza pendekezo la mpango wa kujitathimini wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2016, kwa kuridhia mkataba wa nyongeza wa haki za raia na siasa na kutangaza kuwa haitekelezi adhabu hiyo. Alisema Tanzania inapaswa kujifunza kutoka kwa mataifa mengine duniani ambayo hayatekelezi adhabu ya kifo. Henga alisema  badala yake hutoa adhabu mbadala kama vile kifungo cha maisha na kazi ngumu kwa watuhumiwa wa mauaji ili kulinda haki ya msingi ya kuishi. “Kama watetezi wa haki za binadamu tunampongeza Rais Magufuli kwa kuweka wazi msimamo wake wa kutounga mkono adhabu ya kifo,”alisema Henga. Alisema LHRC inapinga kuondolewa adhabu hiyo kwa sababu ni ya ukatili na isiyo na staha, inayotoa utu wa binadamu na inayofanya Serikali ionekane ni mhalifu kwa kuua. “Hii ni adhabu ya ubaguzi maana mara nyingi wanaopatikana na hatia na kupewa adhabu ni masikini wasioweza kuwa na uwakilishi na ushauri wa sheria,”alisema Henga. Alisema adhabu ya kifo inavunja misingi ya tamko la kimataifa la haki za binadamu la mwaka 1948 ambalo linaeleza kuwa kila mtu ana haki ya kuishi. Alisema hadi sasa hakuna ushahidi kuwa kuwapo adhabu hiyo unasaidia kupunguza uhalifu badala yake mauaji yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku. Alisema kwa mujibu wa ripoti ya haki za binadamu ya mwaka 2016, takwimu zinaonyesha hadi mwaka 2015 kulikuwa na watu 472 waliohukumiwa kunyongwa, kati yao wanaume wakiwa 452 na wanawake 20. Pia, kati ya hao wanaosubiri kunyongwa ni 228, huku 244 wakisubiri uamuzi wa rufaa zao. Alisema taarifa ya haki za binadamu ya mwaka 2016 inaonyesha kuwa Tanzania ilikuwa na   watu 472 wanaume wakiwa 452 na wanawake 20, ambao walihukumiwa kunyongwa, kati yao  228 wanasubiri kunyongwa na wengine 224 wanasubiri uamuzi wa rufaa zao. “Licha ya adhabu hii kutotekelezwa nchini tangu mwaka 1994,  Mahakama imeendelea kutoa hukumu hii ya kinyama na isiyokubalika kwa wote wanaoheshimu haki za binadamu na utu wa mtu,” alisema. Alisema kutokana na mfumo wa sheria nchini kuwa na mianya mingi ya makosa ni vigumu kuwa na uhakika kuwa haki itatendeka wakati wa upelelezi, ubambikwaji kesi, changamoto za upelelezi na waendesha mashtaka kuweza kufanya makosa. “Tunapenda kuweka wazi kwamba hatukubaliani na vitendo vyovyote vya mauaji na kwa namna hiyo hiyo tusingependa kuona muuaji anauawa baada ya kuua, kufanya hivyo ni kuhalalisha kifo, kukubaliana na wauaji na kuondoa kabisa utu wa mtu. “Serikali itekeleze pendekezo la mpango wa kujitathimini wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2016 kwa kuridhia mkataba wa nyongeza wa haki za raia na siasa na kutangaza rasmi kuwa haitekelezi adhabu ya kifo,” alisema.
3
RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Leah Ulaya, amesema migomo na maandamano ya wafanyakazi katika kudai stahiki zao si suluhisho la mwisho kupata haki zao.Ulaya alisema hayo jana kwenye mkutano wa Shirikisho la Vyama vya Walimu vya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEATU), unaofanyika jijini hapa. Alisema migomo na maandamano, siyo njia sahihi ya kupigania haki na sio utaratibu, utakaohitimisha upatikanaji wa stahili kama vyeo na mishahara dhidi ya waajiri, bali ni vurugu ambazo mwisho zitapatiwa suluhisho katika meza ya mazungumzo kwa pande zote.Alisema alijifunza kwa migomo ya walimu iliyofanyika nchini Kenya hivi karibuni, ambayo ilichukua muda mrefu na mwisho wa siku walimu hawakupata suluhisho la madai yao. Badala yake, mwajiri aliwaambia hawakuwa kazini hivyo hana mshahara wa kuwalipa.“Wenzetu wa Kenya walikuwa na madai mbalimbali ya stahiki zao wakagoma kwa takribani mwezi mmoja, matokeo yake mwajiri ambaye ni serikali akawaambia sina pesa za kuwalipa kutokana na kutofanyakazi kwa muda mrefu, mambo haya si suluhisho la kufikia waliyoyataka, njia nzuri ni meza ya mazungumzo,” alisema.Rais huyo wa CWT alisema uzoefu alioupata kupitia vikao vya shirikisho la FEATU, umemsaidia kuona Tanzania kuna mafanikio kwa madai ya stahiki za kupanda madaraja, baada ya kukaa mezani na mwajiri na kuweka mkataba wa maridhiano na baadaye serikali, ambaye ni mwajiri mkuu kutekeleza madai hayo.“Umoja wetu wa FEATU kwa Afrika Mashariki uko bega kwa bega na Shirikisho la Kimataifa la Elimu la Afrika (EIA) na Chama cha Walimu cha Denmark (DLF) ambao ni wafadhili wa FEATU pamoja na Shirika la Kazi Duniani (ILO),” alisema.Mratibu wa FEATU ambalo makao yake makuu yapo Arusha, Anthon Mtavangu alisema shirikisho hilo limeshapeleka maombi ya kupewa fursa ya kushiriki katika masuala ya elimu.Aidha, Mtavangu alitaja madhumuni ya shirikisho hilo kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa ni kuunga mkono juhudi za jumuiya hiyo na mifumo na michakato ya sera za elimu, kusaidia kutunza, kuthamini na kuunga mkono lugha ya Kiswahili ndani ya shirikisho lenyewe na ndani ya jumuiya. Alisema madhumuni jingine ni kutetea maendeleo na viwango bora katika sekta ya elimu na mambo ya walimu. Alitaja nchi sita zinazounda shirikisho la FEATU kuwa ni Tanzania, Uganda, Zanzibar, Rwanda, Burundi na Kenya.
3
MWANARIADHA nyota wa Tanzania, Alphonce Simbu amewataka viongozi wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) kuacha malumbano, sivyo mchezo huo utaendelea kuporomoka.Akizungumza kwa njia ya mtandao kutoka Doha, Qatar jana baada ya kumaliza katika nafasi ya 16 katika mashindano ya dunia katika marathon, Simbu alisema kutofanya vizuri kwa Tanzania katika mashindano hayo kunatokana na maandalizi duni yaliyosababishwa na uongozi.Simbu, kabla ya mbio hizo za usiku wa kuamkia jana, ndiye alikuwa mshindi wa medali ya shaba ya marathon aliyoipata baada ya kumaliza watatu katika mashindano ya dunia yaliyofanyika London 2017, lakini ameshindwa kutetea medali hiyo.Wanariadha wengine wa Tanzania, Augustino Sulle na Stephano Huche, ambao walishiriki na Simbu marathoni hiyo ya wanaume, waliungana na Failuna aliyekimbia Septemba 27 kutomaliza mbio kutokana na joto kali.Simbu ambaye alimaliza mbio hizo juzi kwa saa 2:13:57 alisema kuwa mwaka huu RT haikusaidia maandalizi ya timu hiyo na hiyo inatokana na mgawanyiko mkubwa uliopo ndani yake, ambao viongozi wa juu hawaelewani.Akizungumza kwa uchungu alisema ni jambo la kusikitisha, kwani malumbano na kutoelewana kwa viongozi hao wa juu wa RT, ndiko kunachangia kwa kiasi kikubwa kuurudisha nyuma mchezo huo, ambao ulishaanza kupanda juu miaka miwili iliyopita.Alisema kuwa kila mtu katika RT anafanya lake na timu hiyo kama waliisusa, tofauti kabisa na huko nyuma, ambapo viongozi walikuwa wamoja na walishirikiana kwa pamoja kuihudumia kambi na wachezaji wa timu ya taifa.Simbu alisema kuwa endapo mgawanyiko huo utaendelea ndani ya shirikisho hilo, basi riadha itaendelea kutumbukia shimoni kama si kupotea kabisa.Akizungumzia mbio hiyo ya juzi, alisema mchuano ulikuwa mkali sana na wale waliojiandaa vizuri ndio wameshinda na aliwapongeza kwa ushindi huo.Amesema hata yeye kama angejiandaa vizuri alikuwa na nafasi ya kumaliza ndani ya tatu bora na kuondoka na medali, lakini kwa kuwa hakujiandaa vizuri, ameshindwa kumaliza katika nafasi za juu.Katibu Mkuu wa RT, Wilhlem Gidabuday, ambaye yuko Doha alipopigiwa simu hakupokea, wakati Rais wa shirikisho hilo, Antony Mtaka alipotafutwa kwa njia ya simu alisema, apigiwe baadae.
4
“TNBC inaendelea vema na maandalizi ya mkutano huo na hivyo wadau wote kupitia Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) watashiriki na kutoa michango yao kwenye mkutano kwa ajili ya kukuza biashara na uwekezaji hapa nchini,” alisema Dk Nagu.Alisema uchumi wa nchi unategemea sekta hiyo na Serikali kazi yake ni kuweka mazingira bora ya sekta hiyo kufanya biashara na uwekezaji katika mazingira yanayochangia kukua kwa biashara zao.Aliongeza kusema mkutano huo ni chombo muhimu cha majadiliano ambapo kila upande utatoa maoni yake kwa nia ya kuboresha shughuli za kiuchumi kwa kutumia rasilimali ambazo nchi hii imejariwa kuwa nazo.“Jukwaa hili ni sehemu muhimu ya kuongelea hasa Sekta Binafsi kwa kuwa wao ndiyo waliobeba dhamana ya kuendesha uchumi wa nchi,” alisisitiza.Alisema mkutano hutumika pia kuzungumzia changamoto mbalimbali zikiwemo za vijana wengi kutokuwa na ajira ambapo sehemu pekee ya kukuza ajira hizo ni kuimarisha Sekta Binafsi iweze kutoa ajira nyingi kwa vijana.“Nchi ina ardhi nzuri kwa kilimo, madini, mbuga za wanyama, bandari na Mlima Kilimanjaro, gesi na shughuli za utalii na baadaye mafuta, tukiweza kuzitumia kwa mafanikio tunaweza kupiga hatu zaidi ya nchi kama Singapore,” alisisitiza.Waziri Nagu, alisema Benki Kuu (BoT) na Wizara ya Fedha zinahitajika kuona namna ya kuimarisha taasisi za fedha ili sekta hiyo iweze kupata mikopo ya kuendeleza biashara na uwekezaji.Alisema ili Tanzania iweze kufikia malengo yake inahitajika kuwa na viwanda vya kisindika mazao yake na kulitumia soko lenye jumla ya watu milioni 700 katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika,(SADC), na Jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki (EAC).Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bazara, Raymond Mbilinyi alisema Taifa lina kila aina ya utajiri wa kuweza kupiga hatua kiuchumi, hivyo mkutano huo ndiyo sehemu ambayo wadau watapata fursa ya kuzungumza masuala hayo.“Sisi kama Baraza tumejiandaa vizuri na maandalizi yake yamekamilika,”alisema na kuongeza kuwa wataalamu mbalimbali wameandaliwa kutoa mada.
5
['Mchezaji nyota wa Liverpool Sadio Mane ameisaidia Senegal kutinga robo fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) baada ya kuilaza Uganda bao 1-0.', 'Bao hilo la ufunguzi lilitiwa wavuni na Mane katika dakika za mwanzo wa kipindi cha kwanza liliashiria mwanzo mzuri kwa Senegal katika kampeini yake kuelekea fainali ya kipute hicho. ', 'Timu hiyo imeonesha mchezo mzuri tangu mwanzo wa mashindano haya japo ilinyukwa na bao 1-0 na Algeria katika mechi ya makundi.', 'Mchezaji Idrissa Gueye - anayesakata soka ya kulipwa katika klabu ya Everton alionesha uhodari wake katika mechi hiyo kwa kudhibiti safi ya kati peke yake na kuongoza kasi ya mchezo kwa wachezaji wenzake.', 'Uganda ilifanya makosa mengi na kukosa uwezo wa kiufundi wa kudhibiti mchezo huo. Uganda pia ilifanya makosa mengi ya ulinzi katika mashindani ya kiwango hiki iliyosababisha wafungwe bao huku Mane akipoteza penati dhidi yao.', 'Uganda imeondolewa katika mashindano hayo lakini wachezaji wake waliiweka taifa hilo mbele kwa kuonesha mchezo mzuri na pea talata ya wachezaji wake.', 'Senegal imeondoa timu zote za Afrika Mashariki ambapo ilianza na Tanzania, Kenya na sasa Uganda. ', 'Kwa upande wake Benin iliichapa Morocco mabao 4-1 kupitia mikwaju ya penati na kujikatia tiketi ya robo fainali ya michuano hiyo.', 'Mama Seibou ndiye aliyeweka kimyani penati ya ushindi na kuisogeza mbele timu ya Benin iliyokuwa na wachezaji 10 baada ya Khaled Adenon kutolewa uwanjani katika muda wa ziada wa mchezo huo.', 'Katika mechi hiyo ya kusisimua uliyochezwa mjini Cairo, Moise Adilehou aliiweka Benin kifua mbele kabla ya Youssef En-Nesyri kusawazisha bao hilo.', 'Morocco walikua na nafasi ya kushinda katika muda wa kawaida lakini penati ya Hakim Ziyech iligonga mlango wa goli na mpira ukatoka nje.', 'Benin walifunga penati zao zote kupitia wachezaji Olivier Verdon, David Djigla na Tidjani Anaane kabla ya juhudi za Seibou kukamilisha mechi hiyo kwa shangwe kubwa nje na ndani ya uwanja wa Al Salam.', 'Benin ambao wanashiriki kwa mara ya nne mashindano ya Afcon sasa watakipiga na Senegal katika awamu ya ribo fainali itakayochezwa Julai 10.']
4
MKUU wa Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Sophia Mjema, ametoa mwito kwa wazazi wapunguze muda wa matumizi ya mitandao ya kijamii ikiwemo ya  WhatsApp na Instagram, badala yake watumie muda mwingi kuwa karibu na watoto wafahamu maendeleo yao kitaaluma.Ametoa mwito huo wakati wa mahafali ya darasa la saba kwenye Shule ya Msingi Tusiime ya Tabata jijini Dar es Salaam. Mjema amesema wazazi na walezi wengi wamepunguza mapenzi na ukaribu kwa watoto wao kutokana na kutumia muda mwingi kwenye mitandao hiyo.Amesema hatua ya wazazi na walezi hao kutumia muda mwingi kwenye mitandao hiyo kumesababisha watoto kuwa wapweke na kukosa watu wa kuwafuatilia maendeleo yao hasa ya kitaaluma.“Unakuta baba au mama yuko chumbani anaona shida hata kwenda kujumuika na wenzake kula chakula, anasema nileteeni chakula huku huku chumbani na ukiangalia hakuna cha maana sana anachofanya zaidi ya kuwa na simu. Sasa tabia hii inapunguza upendo kwenye familia,” amesema Mjema.Ameipongeza Tusiime kwa namna ambavyo imekuwa ikifaulisha wanafunzi wengi kuanzia shule ya awali, msingi na sekondari kwenye matokeo ya kitaifa.“Kwa kipindi cha miaka zaidi ya kumi mfululizo shule hizi zimekuwa zikiongoza katika ngazi ya kata, mkoa na pia kushika nafasi za juu kitaifa, kwetu sisi washauri wa elimu Wilaya ya Ilala hili ni jambo la kujivunia kuwa na taasisi yenye kutekeleza sera ya elimu bila matatizo,” alisema.Amesema Serikali inatambua mchango wa shule hiyo katika makuzi na malezi ya watoto kupitia elimu na malezi bora wanayotoa na kuwataka viongozi wa Tusiime kuendelea kuimarisha mifumo ya usimamiaji ubora. Mkuu wa shule hiyo, Philbert Simon, ameishukuru Serikali kupitia ofisi ya elimu kata, wilaya, mkoa na Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kwa kuwapa miongozo mbalimbali tangu kuanzishwa Tusiime, hivyo kuwafanya wajiamini katika kazi zao.“Pia tunaishukuru serikali kwa kututunuku vyeti na nishani mbalimbali kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo, ikiwa ni ishara ya kutambua na kuthamini mchango wa shule za Tusiime wa kusaidia jitihada za serikali kuelimisha vijana wetu,” amesema.Amesema tangu kuanzishwa kwa shule hiyo miaka 22 iliyopita imepata mafanikio ambayo ndiyo kiini cha shughuli zao shuleni hapo na wameendelea kufanya vizuri kitaaluma kupitia mitihani ya ndani, mitihani ya kata, wilaya, mkoa na kitaifa.“Mfano mwaka jana katika matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi tuliweza kushika nafasi ya 20 kati ya shule 16,545, shule yetu ilishika nafasi ya tatu kimkoa na nafasi ya kwanza Wilaya ya Ilala na mwanafunzi bora kitaifa alitoka hapa Tusiime,” amesema.
3
Na ADAM MKWEPU-DAR ES SALAAM MCHAMBUZI maarufu wa soka nchini, Ally Mayay, amewatoa hofu mashabiki na wanachama wa Simba baada ya kusema anaamini kocha wao, Joseph Omog, atawapa mafanikio.   Simba ilizindua kampeni zake za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu kwa ushindi mnono wa mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kutoka suluhu na Azam katika mchezo wa pili.   Suluhu hiyo iliwatia unyonge wapenzi wa Simba kutokana na kuamini timu yao ina kikosi imara ambacho kina uwezo wa kumtwanga mpinzani wao yeyote kutokana na kusajili wachezaji wenye ubora msimu huu.   Akizungumza na MTANZANIA jana, Mayay ambaye ni kiungo wa zamani wa Yanga, alisema hana shaka na mfumo unaotumiwa na Omog, isipokuwa timu hiyo inahitaji muda wa kutosha wa kujijenga kabla ya kuwa na mwendelezo wa matokeo mazuri.   “Mfumo wa kutumia viungo wengi na mshambuliaji mmoja wa Simba si mpya, Omog ameukuta na hauna tatizo lolote, ni suala la kupewa muda ili ufanye kazi inavyotakiwa.   “Sioni tatizo lolote Simba kwa sasa maana wamefanya usajili wa wachezaji zaidi ya 10, kila mmoja ametoka katika timu iliyokuwa ikicheza mfumo tofauti, kwa hiyo subira inahitajika kabla ya kuwa na mashaka na uwezo wa kocha,” alisema Mayay.   Mayay alisema uongozi wa klabu hiyo utafanya kosa kubwa endapo utaamua kufanya mabadiliko katika benchi lao la ufundi.   “Utakuwa uamuzi wa hatari utakaoharibu kila kitu, timu imeanza msimu vizuri, ingawa wapo wanaokosoa mbinu za mwalimu Omog jambo ambalo nalipinga vikali.   “Hakuna jambo lolote zuri linalokuja kwa haraka, kama suala ni mfumo, Omog anajitahidi kuijenga Simba kulingana na uhalisia wa wachezaji alionao,” alisema Mayay.  
3
HATIMAYE Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limekamilisha agizo la Rais John Magufuli la kujenga nyumba za makazi ya Askari Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam.Awali, nyumba hizo zilikuwa zikijengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) tangu mwaka 2016 kwa gharama ya Sh bilioni 10 na baada ya ujenzi huo kusuasua, ndipo Machi mwaka huu, Rais Magufuli aliamua kuwakabidhi JWTZ kukamilisha kazi hiyo.Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge, alisema jana kuwa jeshi limeshakamilisha ujenzi wa nyumba hizo tangu Oktoba 15 mwaka huu ambazo ni maghorofa 12. Kukamilika kwa ujenzi wa maghorofa hayo kunatoa fursa kwa familia 172 za askari na maofisa magereza kuishi ndani yake. Brigedia Jenerali Mbuge alisema wakati wowote atakwenda kuzikagua nyumba hizo na akijiridhisha atampa taarifa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF) Jenerali Venance Mabeyo, ili naye azikague na kisha amwombe Rais Magufuli aweze kuzifungua rasmi.Alisema japo alimwahidi Rais Magufuli kuzikamilisha nyumba hizo katika kipindi kisichozidi miezi miwili na nusu tangu akabidhiwe Machi 16 mwaka huu, lakini kutokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha haikuwezekana kukamilisha ujenzi ndani ya muda aliosema. Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa JKT, kama nyumba hizo zingejengwa kama alivyotaka Rais Magufuli tangu mwanzo, zingeweza kuchukua familia 326. Wakati alipotembelea ujenzi wa nyumba hizo Machi 16 mwaka huu, Rais Magufuli alichukizwa na kitendo cha TBA kushindwa kukamilisha ujenzi kwa zaidi ya miaka miwili tangu wakabidhiwe kazi hiyo mwaka 2016.Kutokana na hali hiyo, aliamua kuwafukuza TBA na kuliagiza JWTZ kukamilisha ujenzi wake. Wakati huo akiwa na Cheo cha Kanali ambapo kwa sasa ni Brigedia Jenerali, Mbuge alimhakikishia rais kuwa jeshi lingeifanya kazi hiyo usiku na mchana na kuikamilisha si zaidi ya miezi miwili na nusu kwa kuwa jeshi halishindwi kitu.“Mimi kwenye serikali nataka kazi, siwezi kwenda kwenye ‘site’ halafu hakuna chochote kinachofanyika tangu mwaka 2016, haiwezekani, si kwa wakati wangu, kuanzia leo, watu wa TBA nimewafukuza, msionekane hapa, nitafanya tathmini ya pesa yangu niliyoitoa Sh bilioni 10 nijue imetumika wapi, ili kusudi kama walitumia vibaya wazitapike, na watazitapika kweli,”alisisitiza Rais Magufuli. Akaongeza:“Sasa Kanali (kwa sasa ni Brigedia Jenerali), kuanzia leo, hii ‘site’ nimewakabidhi Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), TBA nimewafukuza hapa, nimewaleta ninyi msimamie hapa, asiwabughudhi mtu yeyote, mkishamaliza kazi, nitakuja niwakabidhi Magereza.”Kabla ya kuwakabidhiwa kazi hiyo, alilisifu JWTZ kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kujenga ukuta kuzunguka mgodi wa Mirerani mkoani Manyara pamoja na ujenzi wa nyumba 45 za Makao Makuu Dodoma Baada ya maagizo hayo, alimtaka Birigedia Jenerali Mbuge kumweleza mpango kazi wake utakavyokuwa. Katika maelezo yake, alimhakikishia rais kuwa siku iliyofuata ya Machi 17 angewapeleka wataalamu kwa ajili ya kuanza ujenzi mara moja na wangeifanya kazi hiyo usiku na mchana.
3
NCHI za Kiafrika zimeiomba China kuhakikisha kuwa ufadhili ama mikopo inayotoa kwa nchi hizo inalenga katika miradi ya kikanda itakayoziunganisha na kuzinufaisha nchi hizo kiuchumi.Tanzania imeitaka China kuhakikisha kuwa miradi ya maendeleo inayowekeza nchini iwe ya manufaa kwa pande zote mbili.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi aliyasema hayo Beijing, China katika mkutano wa waratibu wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Afrika (FOCAC) alipopata fursa ya kuzungumza katika mkutano huo.Alisema endapo China itazisaidia kwa ufadhili ama kwa mikopo nafuu kuwekeza katika miradi hasa ya miundombinu itakayoziunganisha nchi za kiafrika kwa kiasi kikubwa itazisaidia nchi hizo kufanya biashara zenyewe kwa zenyewe itaziwezesha kupiga hatua za kimaendeleo na kiuchumi na hivyo kujitegemea.Aliongeza kuwa mkutano huo wa FOCAC umekuwa ni wa manufaa kwa kuwa nchi zenyewe za kiafrika zimepata fursa ya kutaja baadhi ya miradi ya kipaumbele kutokana na uhitaji wa nchi husika huku akiitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji kwa kuwa nchi nyingi za Kiafrika bado zina vyanzo vingi vya maji vinavyoweza kuzalisha umeme ambao utakuwa ni wa bei nafuu na kusaidia katika ujenzi wa viwanda.Aidha katika mkutano huo wa siku mbili nchi 53 za Kiafrika zimeitaka China pia kuhakikisha inasaidia ama kufadhili katika kuinua uwezo wa kitaaluma utakaowawezesha vijana kwa Kiafrika kujiajiri na kupata wataalamu wabobezi katika masuala mbalimbali kutokana na uwekezaji hasa wa viwanda na miundombinu utakaofanywa kwa pamoja na China na nchi za Kiafrika.Akizungumza baada ya kumalizika kwa mkutano huo, Profesa Kabudi alisema Tanzania imesisitiza kuwa katika miradi ya uwekezaji ya misaada ama ile ya mikopo nafuu inayoelekezwa Tanzania iwe ni ile yenye manufaa kwa pande zote mbili kama anavyosisitiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli.
3
Kinondoni ni wilaya maarufu sana hapa nchini, wenyewe wanapaita kuwa kwa wajanja na wala bata wa mjini Dar es Salaam. Msimu uliopita katika kigi kuu Vodacom Tanzania bara wanjanja hao waliingiza timu moja ikitokea ligi daraja la kwanza ambayo inatwa KMC. Iliwavuruga sana vigogo wa ligi hiyo pendwa Afrika mashariki na kati kwani KMC ilikuwa inatembeza kichapo bana ilifanikiwa mpaka kucheza mashindano ya Shirikisho Klabu bingwa Afrika. Hivi karibuni imekuwa na matokeo mabaya sana timu hiyo ikiwa imecheza michezo 23 kati ya 38, isipokuwa makini inaweza kujikuta inashuka Daraja si unajua saivi zinashuka timu 6 bana. KMC ambayo ipo nafasi ya 17 katika msimamo huo wa Ligi Kocha wao amewarushia lawama wachezaji akisema wachezaji wakiingia uwanjani wanasahau maeelekezo. Haruna Hererimana ambaye ndiye kocha wa timu hiyo ilipogiwa goli mbili kwa bila jana ikicheza na Namungo anasema wakati mwingine analazimika kufoka lakini jambo la usahaulifu ndilo libaloitafuna timu. “Wachezaji wakiingia uwanjani wanasahau maelekezo” – Kocha wa KMC, Harerimana Haruna akieleza kinachoitafuna timu yake baada ya kufungwa 2-1 na Namungo FC kwenye mchezo wa jana. asema inamlazimu kufoka wakati wa mapumziko ili wachezaji waamke. #LigiKuuTanzaniaBara #VodacomPremierLeague #VPLUpdates #VPL A post shared by Azam Sports (@azamsports2) on Feb 19, 2020 at 2:53am PST
1
Tofauti na matarajio ya wengi walioipa Mtibwa nafasi kubwa ya kushinda lakini hali ilikuwa tofauti kwani timu zote zilicheza soka safi kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa mchezo.Aliyewakosesha Mtibwa ubingwa jana alikuwa Vincent Barnabas aliyekosa penalti ya mwisho iliyopanguliwa na kipa wa Simba Ivo Mapunda.Barnabas hajawahi kukosa penalti katika michuano hiyo, ambayo Mtibwa Sugar ilifuzu hatua ya fainali kwa mikwaju ya penalti 7-6 dhidi ya JKU.Waliopata penalti kwa upande wa Simba ni Awadh Juma, Ramadhan Kessy Isihaka Hassan na Danny Sserunkuma huku Shaaban Kisiga penalti yake ikipanguliwa na kipa wa Mtibwa Saidi Mohamed.Simba ilicheza kwa presha dakika mbili za mwanzo na kuwachanganya Mtibwa huku Haruna Singano akikosa bao katika dakika ya pili. Wachezaji wa Mtibwa waliopata penalti ni Ali Lundenga, Shaaban Nditi, na Ramadhani Kichunga, huku Ibrahim Jeba penalti yake ikigonga mwamba na Barnabas ikipanguliwa na kipa Mapunda.Baada ya dakika chache Mtibwa walitulia na kuanza kushambulia lango la Simba na dakika ya 9 mchezaji wa zamani wa Simba Mussa Hassan Mgosi alikosa bao akiwa na kipa Manyika Peter lakini akapiga nje. Dakika ya 44, Mgosi aliikosesha Mtibwa bao baada ya kupaisha mpira akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga.Sekunde chache baadaye, Said Ndemla aliikosesha Simba bao baada ya kupiga mpira nje akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga. Timu hizo ziliendelea kucheza hivyo mpaka dakika tisini ambapo zilitoka sare ya bila kufungana na ndipo ilipoamuliwa zipigiane penalti.
4
['Mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi ametia saini kandarasi ya muda mrefu na Liverpool. ', 'Raia huyo wa Ubelgiji, mwenye umri wa miaka 24, alijiunga na Liverpool kutoka Lille 2014 kwa mkataba wa miaka mitano kabla ya kuhudumu misimu miwili kwa mkopo. ', 'Lakini alirudi na matokeo mazuri akifunga mara mbili dhidi ya Barcelona katika nusu fainali ya kombe la mabingwa wa Ulaya kabla ya kufunga goli la ushindi dhidi ya Tottenham katika fainali ya kombe hilo. ', "''Hisia zangu ni kwamba nilitaka kusalia katika klabu hii . Kuna kitu maalum kinachoendelea hapa''.", 'Manchester City wanakaribia kumsaini mchezaji wa Uhispania Rodri kutoka klabu ya from Atletico Madrid kwa dau litalakovunja rekodi ya klabu hiyo la £62.8m baada ya kulipa ada ya kumuachilia kulingana na timu hiyo ya Uhispania.', 'Atletico imesema kuwa wakili wa mchezaji huyo na wawakilishi wa City walilipa ada hiyo ya kuwachiliwa kwa mchezaji huyo siku ya Jumatano. ', 'Rodri mwenye umri wa miaka 23 tayari amevunja mktaba wake na Atletico ambao ulitarajiwa kukamilika ,mwezi Juni 2023. ', 'Itaipiku rekodi ya awali ya City ya £60m wakati walipomsaini Riyad Mahrez mwaka 2018.', 'Rodri alijiunga na Atletico mnamo mwezi Mei 2018 baada ya kuhudumu miaka mitatu katika klabu ya Villarreal na aliichezea kwa,mbau hiyo mara 34.', 'Tottenham imesajili kiungo wa kati wa Ufaransa Tanguy Ndombele kutoka klabu ya Lyon kwa dau lililovunja rekodi la £53.8m .', 'Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 ametia saini kandarasi ya hadi 2025 na dau hilo huenda likaongezeka hadi Yuro 70m akiongezewa marupurupu. ', 'Rekodi ya uhamisho ya awali katika timu hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Davinson Sanchez aliyesajiliwa kutoka Ajax kwa dau la £42m. ', 'Ndombele alijiunga na Lyon 2017 na kuisaidia kumaliza katika nafasi ya tatu katika ligi ya Ufaransa msimu uliopita.', 'Pia alicheza mara mbili dhidi ya Manchester City katika mechi za raundi ya muondoani za kombe la mabingwa Ulaya.', 'Manchester United imemsaini mchezaji wa Uingereza na beki wa kulia wa Crystal Palace Aaron Wan-Bissaka kwa dau la £50m .', 'Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 ambaye aliichezea Palace mara ya kwanza mwaka uliopita amekubali kutia saini kandarasi ya miaka mitano ambayo itamfanya kupokea £80,000 kwa wiki.', 'United tayari imelipa £45m mapema , na kumfanya Wan-Bissaka kuwa mchezaji wa tano aliyesainiwa kwa dau kubwa , baada ya Paul Pogba, Romelu Lukaku, Angel di Maria na Fred. ', 'Man United ilithibitisha usajili wake siku ya Jumamosi', 'Mkufunzi Ole Gunnar Solskjaer alisema kuwa Wan-Bissaka alikuwa beki bora anayechipuka katika ligi ya Premia.', 'Arsenal imekamilisha uhamisho wa kwanza msimu huu baada ya kumsaini kinda wa Brazil Gabriel Martinelli.', 'Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 18 ametia saini kandarasi ya muda mrefu , Arsenal imethibitisha. ', 'Martinelli amejiunga na Arsenal kutoka klabu ya Ituano ambapo alikuwa amefunga magoli 10 katika mechi 34 baada ya kuanza kuichezea klabu hiyo ya Brazil 2017.', "''Nataka mchezo wangu kufanana na ule wa Ronaldo'', alisema Martinelli.", 'Ni mchezaji ambaye anafanya kazi kwa bidii akiweka juhudi za kuafikia malengo yake. Kila mara anapigania kushinda mataji.', 'Mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford ametia saini makubaliano ya mshahara wa £200,000 kwa wiki ili kusalia katika klabu hiyo hadi mwezi June 2023, akiwa na fursa ya kuongeza mkataba wake kwa mwaka mmoja. ', 'Mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 21 alijiunga na United akiwa na umri wa miaka saba kabla ya kuanza kukichezea kikosi kikuu cha timu hiyo 2016 akiwa na umri wa miaka 18.', 'Chelsea imemsaini kiungo wa kati wa Croatia Mateo Kovacic kutoka Real Madrid kwa dau la £40m, licha ya kuhudumia marufuku ya miaka miwili.', 'Kovacic alihudumu misimu miwili iliopita kwa mkopo akiichezea The Blues , akiwasaidia kushinda kombe la Yuropa na anajiunga kwa mkataba wa miaka mitano. ', 'Chelsea tayari iliukuwa imemsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 wakati alipokuwa kwa mkopo hivyobasi hakuhitaji usajili upya. ', 'Marufuku hiyo ya uhamisho iliotolewa na Fifa itahudumu hadi 2020 Januari.', 'Manchester United wamemuongezea kipa wa Uhispania David de Gea mashahara katika harakati za kumrai kusalia katika timu hiyo.', 'Mkataba wa De Gea unakamilika baada ya miezi 12 na juhudi za kumfanya mchezaji huyo kutia saini kandarasi mpya zimegonga mwamba.', 'Inajulikana kwamba ofa iliotolewa na Man United itamfanya kuwa kipa anayelipwa zaidi dunini.', ' Karibia ajiunge na Real Madrid 2015.']
4
Wazee wa Chama cha ACT Wazalendo, Mkoa wa Kigoma, endapo Spika wa Bunge, Job Ndugai atatekeleza azma ya  kumkataza Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuzungumza bungeni watamshtakia Mungu. Pamoja na mambo mengine, wazee hao wamesema wamesikitishwa na kauli hiyo ya Spika na wamemruhusu Zitto kuhojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge baada ya kumsikiliza kwa kina na kujiridhisha. “Baada ya kusikia kauli za Spika dhidi ya Zitto, tulihitaji kufahamu sababu na kiini cha tatizo lililotokea, hivyo tulimuomba kijana wetu kurejea nyumbani Kigoma kuja kutueleza kabla ya kwenda kwenye kamati ili tupate fursa ya kufahamu kilichotokea,” imesema sehemu ya taarifa ya wazee hao. Kwa mujibu wa taarifa yao waliyoitoa leo Septemba 15, wazee hao wamekwenda mbali zaidi kwa kusema kitendo cha Spika kutoa kauli ya kumzuia Zitto kuzungumza katika kipindi chote cha ubunge wake ni kuwazuia wao na wananchi wa Kigoma kusemewa ndani ya bunge. “Kitendo cha Spika kutoa kauli hiyo kinaashiria kwamba ameshamhukumu mbunge na kiongozi wetu, kwa hivyo kuitwa kwake kwenye kamati ni kupoteza wakati tu, jambo hili halimtendei haki kijana wetu na halitutendei haki sisi wazee tunaomtegemea atusemee. “Tumesikitishwa na kauli za Spika Ndugai kwani siku zote sisi wazee wa Kigoma tumekuwa tukimuona na kumchukulia Job kama alivyo mtoto wetu Zitto, wawili hawa wamekuwa na mahusiano mema hata kufikia hatua ya kushiorikiana kwa karibu kwenye mazishi ya mama zao,” wamesema wazee hao. Spika Ndugai alitoa kauli ya kutishia kumzuia Zitto bungeni kwa kipindi chote cha ubunge wake na asiende popote wakati akizungumza bungeni wiki hii kwa kile alichodai Zitto amemdhalilisha Spika na Bunge kuhusu ripoti ya Tanzanite na Almasi kuwasilishwa serikalini.
3
Bakari Kimwanga -Dar es Salaam KAMISHNA wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Freddy Manongi, amesema kuna mafanikio katika kupambana na ujangili kwani katika kipindi cha miaka minne hakuna tembo wala faru aliyeuawa na majangili. Manongi alisema hayo jana Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza kwenye programu maalumu kwa waandishi wa habari kutoka Thailand na Tanzania, iliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET) kwa ufadhili wa USAID-Protect. “Hili kwetu tunajivunia sana kwani katika miaka minne ya uongozi wa Rais John Magufuli kwa kweli hakuna mzoga wa tembo ambao nimeukuta katika eneo la mamlaka au hata kuripotiwa kwenye hiafadhi nyingine nchini kwamba kuna mnyama kauawa na majangili. “Hata ukiona tembo amekufa basi ni kwa mambo mengine, lakini si ujangili. Hivyo imefanya kuongezeka wanyama wetu jambo ambalo ni la kujivunia,” alisema Dk. Manongi. Pamoja na hali hiyo, alisema licha ya juhudi zinazochukuliwa na Serikali, bado jamii inatakiwa kunufaika na mapato yatokanayo na hifadhi. Alisema pamoja na Mamlaka ya Ngorongoro kupata mafanikio, mwaka 2017 kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), walifanya sensa ya watu na wanyama ambapo ilibainika changamoto kadhaa ikiwamo ongezeko la shughuli za watu zaidi ya 95,000 katika eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. “Idadi ya watu imeongezeka na hili linatokana na mila zinazochangia shughuli za binadamu. Lakini pia idadi ya mifugo inaongezeka hali ambayo imesababisha kuwapo kwa magonjwa toka kwa wanyama kwenda kwa binadamu ikiwamo kimeta na minyoo. “Sensa hii pia ilibanika zaidi ya asilimia 60 ya watu wanaoishi ndani ya hifadhi hawajui kusoma na kuandika. Sasa hii ni changamoto, sisi kama mamlaka tumejenga shule 21 za msingi na za sekondari mbili ambazo zina kidato cha tano na sita. “Pia Serikali imekuwa ikitoa kiwango kikubwa cha fedha kwa ajili ya kugharamia elimu, swala ambalo nasi tunajiuliza je, mfumo wetu na walimu hawana maarifa ya kutosha au nini? Hili ni swali ambalo bado linatuumiza vichwa sana,” alisema Dk. Manongi. Alisema pamoja na hali hiyo bado mamlaka yao imekuwa ikifanya vizuri kwa upande wa mapato ambapo kwa mwaka wa fedha wa 2018/19 walikusanya  Sh bilioni 120 na kupokea wageni wa ndani na nje ya nchi 600,000.
3
ZURICH, USWISI NYOTA waReal Madrid, Cristiano Ronaldo, usiku wa kuamkia jana alifanikiwa kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia ‘Ballon d’Or’ kwa mara ya pili mfululizo, huku mwaka huu akipanga kuchukua tena na kumzidi nyota wa Barcelona, Lionel Messi aliyeitwaa mara nne. Nahodha huyo wa timu ya Taifa ya Ureno aliwapiku wapinzani wake, Messi na kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer, waliokuwa wakishindanishwa kuwania tuzo hiyo. Nyota hao watatu pia walifanikiwa kuorodheshwa kwenye kikosi bora cha mwaka jana cha Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), sambamba na wachezaji wengine mabeki Philipp Lahm, David Luiz, Thiago Silva na Sergio Ramos, viungo ni Andres Iniesta, Toni Kroos na Angel Di Maria pamoja na Arjen Robben, ambaye ni mshambuliaji. Tuzo hiyo inamfanya Ronaldo, 29, kufikisha jumla ya tuzo tatu za Ballon d’Or na kuwafikia magwiji wa zamaniJohan Cruyff, Michel Platini na Marco van Basten waliotwaa idadi sawa kama yeye, huku akiwa na mtihani mzito wa kumfikia Messi anayeongoza kwa kutwaa mara nne. Mara baada ya kutwaa tuzo hiyo Ronaldo alisema:”Nataka kuwa mchezaji mkubwa duniani wa muda wote na hii inahitaji jitihada kubwa, lakini nina imani ya kufika huko…Napenda kuwashukuru mashabiki wangu wote walionipigia kura na wachezaji wenzangu wa Madrid, rais wetu wa klabu na kocha wangu. Bila shaka ulikuwa mwaka wenye mafanikio sana kwetu.” Naye Rais wa Real Madrid, Flolentino Perez, alifurahishwa na tuzo ya mchezaji wake huyo huku akieleza tayari nyota huyo ameshapanga kuitwaa tena mwaka huu na kumfikia mpinzani wake Messi. “Cristiano anataka kuvunja kila rekodi,” alisema. “Anataka kuchukua tuzo ya nne ya Ballon d’Or na anafanya kazi ya kuishinda na ameanza vema mwaka huu, pia kama alivyosema, jambo la muhimu ni timu inacheza vizuri, ni timu kubwa La Liga, inafanya makubwa na kwa yote hayo inakuja tuzo ya mtu binafsi.” Baada ya kumpata mshindi, FIFA ilitoa orodha ya wachezaji 10 walioingia 10 bora ya tuzo hiyo na asilimia za ushindi wao,Ronaldo (37.66%), Messi (15.76%), Neuer (15.72%), Robben (7.17%), Thomas Muller (5.42%), Lahm (2.90%),Neymar (2.21%), James Rodriguez (1.47%), Toni Kroos (1.43%), Angel Di Maria (1.29%). Mbali na tuzo hiyo iliyoteka hisia za watu wengi, FIFA ilitoa nyingine ambazo ni; Mchezaji bora wa kike Kiungo wa klabu ya Wolfsburg na timu ya taifa ya Ujerumani ya wanawake, Nadine Kessler, alitwaa tuzo hiyo akimpiku nyota wa Brazil, Matra na nyota mwingine wa Marekani Abby Wambach. “Moyo wangu unagonga mapigo ya ajabu wakati huu, sikuwahi kufikiri kufika hapa katika maisha yangu, bila ushirikiano wa wachezaji wenzangu na kocha wangu hakika nisingeweza kufika hapa. Shukrani zangu kwa familia na ndugu zangu kwa ushirikiano walionipa katika safari yangu ya soka,” alisema Nadine. Bao bora la mwaka ‘Puskas Award’ Nyota wa Colombia, James Rodriguez, aliibuka kinara wa bao bora la mwaka akiwapita, Stephanie Roche na mshambuliaji wa Manchester United, Robin Van Persie. Rodriguez alipata jumla ya asilimia 42 akifuatiwa na Roche aliyepata asilimia 33 na mshambuliaji wa Man United akiambulia nafasi ya tatu kwa kupata jumla ya asilimia 11 ya kura zote zilizopigwa. Kocha bora wa wanaume Kocha wa Ujerumani,Joachim Low (54) ametwaa tuzo ya kuwa kocha bora wa mwaka akiliongoza taifa la Ujerumani kutwaa taji la dunia lililofanyika nchini Brazil, kwa kuichapa Argentina bao 1-0 kwenye mchezo wa fainali. “Ni heshima kubwa kwangu kwa mafanikio haya niliyoyafikia, nafahamu michuano ya Kombe la Dunia ndio iliyonifikisha hapa hivyo napenda kuchukua tuzo hii kwa niaba ya wote walioshiriki katika kuweka mafanikio ya timu yetu ya taifa ya Ujerumani. Ahsante kwa wachezaji na familia yangu kwa ushirikiano wao kwangu,” alisema Loew. Kocha bora wa wanawake Kocha wa klabu ya Wolfsburg Ralf Kellermann (46) amechaguliwa kuwa kocha bora kwa upande wa soka la wanawake akifanikiwa kuiongoza klabu hiyo kutetea taji lao la Ulaya. “Tuzo hii imekuja wakati muhimu sana kwangu, napenda kutoa shukrani kwa wachezaji na mashabiki wa timu yangu ya Wolfsburg, ni tuzo yetu wote kwa kuwa wote tulikuwa sehemu ya mafanikio,” alisema Kellerman.
4
WATU wanaokunywa kiwango kidogo cha maji ikilinganishwa na chumvi inayotengenezwa mwilini wako katika hatari ya kupata matatizo ya mawe kwenye fi go na mfumo wa mkojo.Hayo yameelezwa na Daktari Bingwa wa Mfumo wa mkojo na upandikizaji wa figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Dk Remigius Rugakingira. Dk Rugakingira aliwaambia maofisa habari wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na taasisi zake katika Kanda ya Kati kuwa matatizo ya mawe kwenye figo na mfumo wa mkojo ni unywaji wa kiwango kidogo cha maji ikilinganishwa na kiwango cha chumvi ambacho mwili unatengeneza.“Kama unakunywa maji kidogo kulinganisha na aina ya chumvi inayotengenezwa mwilini una hatari ya kupata mawe, pia kuwa na bakteria wengi katika mfumo wa mkojo unaweza kutengeneza mawe,” alisema.Dk Rugakingira alisema awali hospitali hiyo ilikuwa ikipokea wastani wa wagonjwa watano kwa mwezi, lakini hivi sasa ni wastani ni wagonjwa 32 kwa mwezi.“Asili ya mawe ambayo tunayaona ni magumu na tuna historia hapa tulitoa jiwe lenye sentimita 4.5 ambalo tumetoa kwenye kibofu, sentimita 2.6 ambalo limetolewa kwenye figo na kuwa na aina hii ya mawe yanaleta shida kwenye njia ya mkojo kama vile kutotoka mkojo wa kutosha,” alisema.Aidha, Dk Rugakingira alisema katika kuboresha utoaji wa huduma, hospitali hiyo inatarajia kufunga mashine mpya ambayo itawasaidia kuyeyusha mawe kwa njia ya kisasa zaidi ambayo itagharimu Sh bilioni sita.“Uwekezaji wa mashine hii ni mkubwa na wa kisasa ni sawa na Ujerumani na nchi zingine, itatumia mionzi kwa hiyo itakuwa unatumia kamera, unaenda kwenye eneo la jiwe na kulivunja, njia nyingine ya pili ni kutumia mfumo wa kufungua, hivyo itatufanya tuwe na uwanja mpana wa kutoa matibabu badala ya kufanya upasuaji wa kuchana,”alisema.Kutokana na ubora wa huduma ambazo wamekuwa wakizitoa wameweza kupata wagonjwa kutoka nje ya Tanzania na kuzitaja nchi hizo kuwa ni Comoro, Saudi Arabia, Ghana na Uganda ambao wamefanyiwa upasuaji wa kuondoa mawe.
3
Mjasiriamali, Sarafina Mohamed, anayeosha miguu ya watu waliochafuka na tope katika Soko la Mabibo (mahakama ya ndizi) akihudumia wateja wake kwa Sh 500, Dar es Salaam jana. Picha na LOVENESS BERNARD     NA TUNU NASSOR, DAR ES SALAAM MVUA inayoendelea katika jiji la Dar es Salaam na kusababisha masoko mengi kujaa tope na uchafu mwingine, imegeuka kuwa fursa kwa vijana na wanawake ambao wamejipatia ajira ya kuosha miguu watu wanaokwenda kununua mahitaji mbalimbali sokoni. Juzi MTANZANIA lilishuhudia watu wanaotoka ndani ya soko la Mabibo maarufu ‘mahakama ya ndizi’ lililopo Wilaya ya Ubungo wakiosha na wengine kuoshwa miguu yao kwa   ujira wa  kati ya Sh 100 na Sh 500.         Mmoja wa wabunifu hao, Sarafina Mohamed, aliliambia MTANZANIA jana kuwa ameamua kufanya kazi hiyo baada ya mvua kuanza kunyesha mfululizo na kuathiri biashara yake ya awali ya kuuza maji ya kunywa maarufu kama ‘maji ya kandoro’ pamoja na sigara. “Kutokana na miundombinu ya soko kuwa mibovu na matope kuwa mengi ambayo yanasababisha wateja kuchafuka, nilibuni njia hii ambayo inanipatia hadi Sh 30,000 kwa siku. Hata hivyo alisema baada ya wenzake kuona anapata wateja wengi, waliamua kumuiga na kuanzisha ‘kijiwe’ kingine kama hicho sokoni hapo.  “Nilikuwa nauza maji ya kandoro na sigara ndani ya soko baada ya mvua kuwa kubwa biashara hiyo ikakosa wateja hivyo nikawa nawaza wateja wanavyotoka sokoni hapa wakiwa wachafu na kuchafua wengine pamoja na magari wanayotumia,” alisema Sarafina. Alisema alianza kama majaribio na ndipo aligundua kuwa kazi hiyo inampa kipato kizuri kila kukicha hasa mvua ikinyesha. “Tofauti na nilivyokuwa nauza maji ya kunywa kipato changu kimeongezeka kwani kwa siku naingiza hadi Sh 30,000. “Mteja akinawa mwenyewe analipia Sh 100 lakini ninapomnawisha analipa Sh 500, hivyo anapokwenda nyumbani au kupanda daladala anakuwa msafi na hachafui wengine,” alisema Sarafina. Alisema amekuwa akinunua maji kwa kila ndoo moja Sh150 na mara nyingi hutumia Sh 9,000 kwa siku kununua maji. “Nimeweza kutoa ajira kwa vijana wanne ambao hunisaidia kufuata maji bombani na wateja wanapokuwa wengi huwanawisha pia,” anasema Sarafina. Alisema kwa kazi hiyo inamsaidia kununua sare za shule za watoto wake na pia husaidia hata chakula kwa familia yake hata kama mume wake atapungukiwa. “Imenijengea uwezo wa kuhifadhi fedha kila siku Sh 20,000 hivyo ninaamini msimu wa mvua ukiisha nitakuwa na fedha nyingi ambazo zitaniwezesha kufanya biashara nyingine kubwa,” alisema.
3
Na LEONARD MANG’OHA-DAR ES SALAAM MAMLAKAya Udhibiti wa Huduma za Nishati na  Maji Tanzania (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei ya petroli huku dizeli na mafuta ya taa vikipanda kwa wastani wa Sh saba hadi 12 kwa lita moja. Bei hiyo ni tofutti ikilinganishwa zilizotangazwa Machi Mosi mwaka huu. Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi   Dar es Salaam  jana ilieleza kuwa bei hiyo itaanza kutumika rasmi hii leo. Taarifa hiyo ilieleza kuwa bei ya rejareja ya petroli imepungua kwa Sh tatu kwa lita moja sawa na asilimia 0.13, huku bei ya jumla ikishuka kwa Sh 5.65 kwa lita au asilimia 0.29. Wakati petroli ikishuka, bei ya dizeli imepanda kwa Sh 12 kwa lita moja sawa na asilimia 0.63, bei ya jumla imeongezeka kwa Sh 9.11 kwa lita sawa na asilimia 0.50. “Bei ya rejareja ya mafuta ya taa imepanda kwa Sh saba kwa lita sawa na asilimia 0.36 ambako bei ya jumla imepanda kwa Sh 3.68 kwa lita sawa na asilimia 0.21. “Kwa kiasi kikubwa, mabadiliko haya ya bei yametokana na mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la dunia, mfumuko wa bei na gharama za usafirishaji (BPS Premiums) ikilinganishwa na mwezi uliopita,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.  Ilisema Machi mwaka huu hakuna mzigo wa mafuta uliyopokelewa nchini kupitia bandari ya Tanga. “Ongezeko hilo la bei za mafuta linatokana na ongezeko la faida ya wauza mafuta wa jumla na rejareja kutokana marekebisho yaliyofanywa kukidhi matakwa ya mfumko wa bei kwa mujibu wa kanuni ya ukokotoaji wa bei za mafuta katika mwaka 2016,” iliongeza taarifa hiyo.
3
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera, amewataka wachezaji wake kuacha utoto na kuongeza nguvu na juhudi katika mapambano ya kusaka pointi tatu kwenye mechi za Ligi Kuu.Mkongomani huyo amekiri timu yake kuzidiwa kimchezo na wapinzani wao Coastal Union licha ya ushindi wa bao 1-0, walioupata kwenye mchezo huo ambao ulichezwa juzi, Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.Akizungumza na gazeti hili, Zahera alisema tatizo kubwa ambalo linasababisha timu yake kuzidiwa kipindi cha pili ni utoto ambao unafanywa na baadhi ya wachezaji wake kwa kuchezea mpira na kuurudisha nyuma kinyume na maelekezo yake.“Tumekuwa tukicheza kwa nguvu na kufunga mabao mwanzoni mwa mchezo, lakini baada ya kupata mabao wachezaji wangu wamekuwa wakifanya utoto mwingi kiasi cha kuigharimu timu na kujikuta tunaruhusu mabao ya kizembe kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Stand United,” alisema Zahera.Kocha huyo alimtaja kiungo Papy Tshishimbi kuwa ni miongoni mwa wachezaji ambao wanashindwa kutimiza ipasavyo majukumu yao kwa kutumia muda mwingi kuuchezea mpira wakati wenzake wapo kwenye nafasi nzuri.Alisema tatizo hilo ataendelea kulifanyia kazi kwenye mazoezi yao ili kulimaliza kabla ya mchezo wao unaofuata dhidi ya Singida United ambao pia wamepania kushinda ili kujiweka kwenye mazingira mazuri ya ushindi.Aidha Zahera amewapongeza wachezaji wake kwa kuvuna pointi tatu nyingine ambazo zimewafanya kuwa na mwanzo mzuri baada ya kushinda mechi tatu mfululizo za kwanza tangu kuanza kwa ligi ya msimu huu.Alisema hiyo imewaongezea ari ya kufanya vizuri kwenye mechi zijazo ambazo licha ya kuamini zitaongeza ugumu kutokana na wapinzani kuwakamia kutokana na matokeo wanayoendelea kuyapata kwenye ligi.“Ni kweli hatukucheza vizuri lakini kitu cha msingi ni pointi tatu ambazo tumezipata tunachofanya ni kuendelea kukumbushana pale kwenye mapungufu na uzuri vijana wangu niwepesi kwenye kushika ninacho waelekeza mazoezini,” alisema Zahera.Kocha huyo ambaye Mkongomani mwenye uraia wa Ufaransa, alisema sababu kubwa iliyochangia timu yake kucheza chini ya kiwango kwenye mchezo dhidi ya Coastal Union ni kukosa muda wa kutosha wa kupumzika ukilinganisha na wapinzani wao.Alisema Coastal walipumzika siku tatu wakati wao walipata siku mbili za mapumziko baada ya mchezo wao na Stand United, jambo ambalo alilijua kama litawaletea shida hasa kwenye kipindi cha pili.
4
Asha Bani, Dar es Salaam Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea anatarajia kupeleka hoja binafsi bungeni kuiomba serikali kuchukua hatua za haraka kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Afrika wa haki za binadamu kuhusu haki za watu wenye Ualbino Afrika. Amesema mkataba huo ulipitishwa katika mkutano wa 30 wa wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika mwaka jana hivyo anaiomba serikali kufanya marekebisho ya sera ya watu wenye ualbino iliyotungwa 2004 ili kuwasaidia kukomesha vitendo vya kikatili dhidi yao. Kubenea amesema hayo leo Jumapili Agosti 11, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa ameamua kuwatetea watu hao kutokana na kulipa deni aliloachiwa na Mwenyekiti wa Kampuni Tanzu za IPP, marehemu Regnald Mengi. “Nimeamua kufanya hivi kutokana na kutaka kulipa deni ambalo nimeachiwa na marehemu Mengi, mimi hili ndiyo deni langu kuenzi alichokuwa anakifanya na si vinginevyo,” amesema Kubenea. Naye Mwenyekiti wa Chama cha Watu Wenye Ualbino Jimbo la Ubungo, Mussa Geuza amesema anawaomba wabunge wengine kumuunga mkono Kubenea kwani hoja yake ina mashiko na ustawi kwao.
3
Alisema hayo wakati akifanya majumuisho mjini Mgumu wilayani Serengeti mkoa wa Mara, baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi, kukagua miradi ya umeme inayosambazwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).Alisema upatikanaji wa gesi kutoka Mtwara, utainufaisha nchi hii kwa kuzalisha umeme kutokana na gesi hiyo na uchumi wa Tanzania utaimarika na kuishinda nchi ya Kenya, ambayo uchumi wake uko juu kuliko wa Tanzania.Alisema Tanzania inataka kuanzisha viwanda vya mbolea, kutokana na gesi na pato la Mtanzania litakuwa kutoka Dola za Marekani 800 (Sh milioni 1.36) kwa kila Mtanzania na kufikia Dola 3,000 (Sh milioni 5.1) kwa kila mwanachi, hivyo Watanzania hawana budi kufanya jitihada za makusudi ili kuinua uchumi wao.“Tunataka kutoka kwenye Tanzania yenye umasikini na kuwa Tanzania yenye uchumi imara, sasa tunatumia umeme kupata uchumi mkubwa katika nchi hii, nawaomba Watanzania tupunguze siasa tufanye kazi ili twende kwenye uchumi imara,” alisema Muhongo.Aliwataka Watanzania kukaa mkao wa kula, kwani bomba la kilometa 542 kutoka Mtwara-Songosongo hadi Dar es Salaam, limekamilika na hivyo Watanzania wataanza kunufaika na umeme ambao utashuka bei.Aliongeza kuwa ifikapo mwaka 2025, Watanzania zaidi watakuwa wanatumia umeme ambapo Serikali itaongeza uzalishaji wa umeme na kwamba Tanzania ndio nchi pekee Afrika Mashariki, ambayo ina mradi wa umeme vijijini.
5
MAADHIMISHO ya Siku ya Nyuki duniani, yameanza kuadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Nyerere Square jijini hapa huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Tuwalinde Nyuki’.Akizungumza katika mahojiano jana, Mkurugenzi Msaidizi Uendelezaji Ufugaji Nyuki kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Allen Richard alisema hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufanya maadhimisho hayo .Alisema lengo ni kuhakikisha jamii inaweza kutambua umuhimu wa nyuki hasa kwenye suala la uchavushaji.“Tunataka wananchi watambue umuhimu wa nyuki katika usalama wa chakula , nyuki ni mdudu anayechavusha vizuri mazao,” alisema.Alisema tafiti zinaonesha asilimia 90 ya mazao yanachavushwa na nyuki na kwa sababu ya shughuli mbalimbali za binadamu, wanatumia viuatilifu kwenye mashamba nyuki, wanaweza kufa na siku za mbele kuna uwezekano wa kukosa makundi ya nyuki .“Kwa kuona hilo tuliona tuwe na siku ya nyuki ili kujenga uelewa kwa jamii juu ya umuhimu wa nyuki kwa ajili ya maisha ya binadamu,” alisema.Alisema wanaelimisha wananchi kutunza mazingira kwa kupanda miti, itakayotumiwa na nyuki kwa ajili ya chakula ili kumuenzi nyuki mwenyewe Richard alisema chimbuko la maadhimisho ya Siku ya Nyuki ni nchi ya Solvenia, ambapo Antonio Janser alikuwa akijishughulisha na ufugaji nyuki na alifanya hivyo baada ya kuona nyuki wanavyofanya kazi zao kwa juhudi na maarifa .Janser alizaliwa mwaka 1734 na alifariki dunia akiwa na miaka 39 baada ya kuugua.Ilipofika mwaka 2012 viongozi wa nchi ya Slovenia waliona ipo haja ya kuwa na Siku ya Nyuki duniani ili kuenzi mchango wa Janser, ndipo wakapeleka mapendekezo kwenye Umoja wa Mataifa na wakapendekeza Mei 20 iwe Siku ya Nyuki duniani.Alisema mwaka jana nchi nyingine zilianza kuadhimisha siku hiyo na Tanzania inafanya maadhimisho hayo kwa mara ya kwanza.Ofisa Uendelezaji Biashara wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Dodoma, Gakune Charles alisema maonesho hayo ni fursa kwa wajasiriamali, kutangaza bidhaa na shughuli wanazofanya.Mmoja wa wananchi waliotembelea maonesho hayo, Abasi Abdallah alisema maonesho hayo yamempa hamasa ya kuanza ufugaji wa nyuki.
3
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza Juni 15, mwaka huu kuwa ni siku ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 32 zilizopo katika halmashauri 20 za Tanzania Bara.Akizungumza ofisini kwake Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Mbarouk Mbarouk alisema kuwa Tume imetangaza tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa, juu ya uwepo wazi wa nafasi 31 za udiwani katika kata 31 za Tanzania Bara kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kujiuzulu na vifo.Aidha, alisema kuwa, Tume imetangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Kitangiri Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza sambamba na kata hizo 31, baada ya Mahakama ya Rufaa kuondoa maombi ya mapitio, yaliyowasilishwa katika Mahakama hiyo, baada ya kutenguliwa kwa matokeo ya uchaguzi wa udiwani katika kata hiyo.Jaji Mbarouk alisema kuwa, fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kati ya Mei 27 na 31, mwaka huu, uteuzi wa wagombea utafanyika Mei 31, kampeni za uchaguzi zitaanza Juni 1 hadi Juni 14, na Juni 15, mwaka huu, ndiyo itakuwa siku ya uchaguzi.Alitaja kata zitakazofanya uchaguzi huo kuwa ni Mto wa Mbu, Mkuyuni na Majengo zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Kata za Ganako, Daa, Mbulumbulu, Oldeani na Kanssay zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Karatu mkoani Arusha na Kata ya Likuyuseka iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.Nyingine ni Kata za Kinyasiti Kati iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na Kata ya Kikombo iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma mkoani Dodoma, Kata ya Itenka iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi, Kata za Ipole na Pangale zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge na Kata ya Itumba iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Igunga za mkoani Tabora.Pia Kata ya Boma iliyopo Halmashauri ya Mji wa Mafinga mkoani Iringa, Kata za Tandika na Chikongola katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara.Katika Mkoa wa Dar es Salaam ni Kata za Bonyokwa iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Kata ya Tungi iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni na Kata ya Chang’ombe iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.Zingine ni Kata ya Ruangwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi, Kata za Mkula na Lamadi zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Busega mkoani Simiyu, Kata za Kibosho Magharibi na Uru Shimbwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi za mkoani Kilimanjaro, Kata ya Murangi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Musoma mkoa wa Mara na Kata ya Siuyu iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.Pia Kata za Kyaitoke, Mugajale na Ruhunga zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera na Kata ya Kitangiri iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imevikumbusha vyama vya siasa na wadau wote wa uchaguzi, kuzingatia sheria, kanuni, maadili ya uchaguzi, taratibu, miongozo na maelekezo yanayotolewa na Tume wakati wote wa kipindi cha uchaguzi huo mdogo
3
KATIKA kuelekea kujitegemea kwa asilimia 100, Jiji la Dodoma linatarajia kuanza ujenzi wa hoteli mbili za kisasa ili kuongeza vyanzo vya mapato vya ndani.Akizungumza jijini hapa, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi amesema muda wowote jiji hilo litaingia mkataba wa ujenzi wa hoteli mbili.“Tutakwenda kusaini mikataba miwili ya kujenga hoteli mbili zenye hadhi ya nyota tatu na nyota tano. Moja itakuwa katikati ya mji na nyingine kwenye mji wa serikali,” alieleza.Kunambi aliongeza: “Miradi hii ina gharama kubwa kupitia mapato ya ndani na miradi hii ni sehemu ya sisi kujitegemea kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2021.”Aidha, Kunambi alisema jiji pia limejiandaa kuja na Kampuni ya Uwekezaji ya Jiji (City Investment Company) ambayo itakuwa na jukumu la kuendesha miradi ya jiji ikiwamo ile mikubwa ya soko na stendi ya kisasa.“Tuna mradi wa soko na stendi, tumejiandaa kisaikolojia na hivi karibuni tunatarajia kutangaza tenda ya kuanzisha kampuni ya uwekezaji,” alisema.Alisema wakiwa kama jiji hawawezi kundesha miradi yote hiyo na kwamba yako yao ya msingi ni kutoa huduma kwa wananchi.“Ndio kazi tunayotaka kubaki nayo tunataka tuwe na kampuni iweze kuendesha miradi mikubwa ya fedha za ndani,” alisema.Mradi wa soko na stendi ya kisasa inayotekelezwa katika jiji la Dodoma ni miongoni mwa miradi inayotekelezwa chini ya Mradi wa Mipango Miji Mkakati (TSCP) inayosimamiwa na Tamisemi, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais kwa kutoa fedha zaidi ya Sh bilioni 77 kujenga miundombinu Dodoma.
5
LEO ni Kumbukizi ya miaka 19 ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki dunia Oktoba 14, 1999 jijini London, Uingereza.Kumbukizi hiyo inaenda sambamba na kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru ambacho sherehe zake kitaifa zinafanyika Uwanja wa Mkwakwani jijini hapa leo.Jana ilikuwa ni kilele cha Wiki ya Vijana ambayo vijana kutoka maeneo mbalimbali ya Halmashauri 11 za Mkoa wa Tanga na sehemu nyingine za nchi, walipata fursa za kuonesha shughuli mbalimbali wanazozifanya katika mabanda ya maonesho yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Tangamano mjini hapa.Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo kinafanya mbio hizo kutimiza siku 195 ambazo uliweka mawe ya msingi, kuzindua, kukagua na kufungua miradi ya maendeleo katika halmashauri 195 za mikoa 31 ya Tanzania Bara na Visiwani tangu ulipozinduliwa Aprili 2, mwaka huu Geita na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ukiwa na ujumbe “Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu.”Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi leo katika sherehe zinazoifanya Tanga iweke historia kwani imepita miaka 10 tangu kilele cha mwisho kifanyike hapo hapo mwaka 2008.Viongozi wengine wa kitaifa wanaotarajiwa kuhudhuria ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai, mawaziri kutoka serikali za Jamhuri ya Muungano na Mapinduzi Zanzibar (SMZ).Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama aliwaambia waandishi wa habari jana maandalizi yote kwa shughuli hiyo yamekamilika.“Pia kesho (leo) Ofisi ya Waziri Mkuu inakabidhi rasmi mpango mkakati wa kutoa ujuzi kwa vijana waweze kujiajiri kwenye sekta ya kilimo kwa kutumia ujuzi na utaalamu mpya kwa kulima mbogamboga na matunda kwenye bustani nyumba maarufu Green House,” alisema.Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa SMZ, Balozi Ali Karume alisema katika sherehe hizo ambazo pia kunakuwa na Wiki ya Vijana, lengo ni kuwaunganisha vijana wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uzalendo wa kujitolea kujenga nchi.Alisema dhumuni la kuuweka Mwenge katika kilele cha Mlima Kilimanjaro ni kumulika nje ya mipaka.Awali, Mkuu wa Mkuu wa Tanga, Martin Shigella alisema maandalizi yote yamekamilika na kuwataka wananchi kuwahi mapema.“Milango itakuwa wazi kuanzia saa 11:30 alfajiri. Maandalizi yamekamilika ikiwemo halaiki, ngoma za utamaduni na wasanii hivyo wananchi mnaalikwa kufika mapema,” alisema.Mwenge huo ulipokelewa Mkomazi wilayani Korogwe ukitokea Kilimanjaro, Oktoba 3, mwaka huu. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira aliukabidhi kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Shigella.
3
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania, Jarson Kalile wakati wa kongamano la wanaushirika Tanzania lililomalizika mwishoni mwa wiki.“Rais John Magufuli aliahidi kuondolea wananchi kodi hasa wa kipato cha chini, ombi letu kwa serikali ni kuangalia upya kodi na mapato mbalimbali kwa lengo la kumpunguzia mkulima mzigo mkubwa wa kodi,” alisema Kalile.Alisema jambo hilo limekuwa kikwazo kikubwa kwa wakulima hivyo harakati zao za kujikwamua kiuchumi kushindwa kuzaa matunda licha ya kutumia nguvu na rasilimali zao chache katika kilimo.“Mathalani katika zao la kahawa kumekuwa na kodi mbalimbali 10 na makato kwenye zao hilo ambapo kwa njia moja au nyingine huathiri bei ya mkulima,” alisema Kalile.Alizitaja kodi hizo kuwa ni pamoja na ushuru wa halmashauri ya wilaya asilimia tano ya bei ya mkulima, ushuru wa utafiti asilimia 0.75 ya bei ya mnadani, mfuko wa maendeleo ya kahawa uliaonzishwa na wadau asilimia 0.5 ya bei ya mkulima, ada ya leseni ya kuuza kahawa nje zinazotozwa na Bodi ya Kahawa (TCB).Pia ada za maghala, leseni, leseni ya kiwanda cha kukoboa kahawa, ada ya kibali cha kuuza kahawa nje kwa njia ya mauzo ya moja kwa moja pasipo kupitia mnadani na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye vifaa mbalimbali vya kuhudumia kahawa yakiwamo magunia.Pia kodi ya mapato (corporate Tax) ambapo kodi hiyo haitakiwi kutozwa kwa wanaushirika kwani faida nyingi inayopatikana ni lazima irudishwe kwa mkulima ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkulima.Kalile alisema hizo ni baadhi ya kodi na makato mbalimbali katika zao lakahawa na hali kama hiyo inajitokeza katika mazao mengine.“Tunapendekeza kodi hizo ziondolewe” alisema. Pia walipendekezwa kuondolewa kwa kodi za VAT kwa kuwa wakulima hulipa kodi hiyo asilimia 18 kwa mazao yao kama kusafirisha kahawa kutoka vyama vya msingi kwenda kiwanda cha kukoboa kahawa, magunia ya kuweka mazao yao na kukoboa kahawa yao kwenye kiwanda.
5
RAIS Salva Kiir amesema yuko tayari kukutana na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), kama akitakiwa kwenda kujibu mashtaka kuhusu uhalifu wa kivita uliotokea wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe.Ripoti ya hivi karibuni iliyotolewa na London School of Hygiene and Tropical Medicine inakadiria kuwa watu 382,900 wamekufa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo vilivyodumu kwa miaka mitano.“Siogopi kwa sababu hakuna kibaya nilichofanya, kama kuna uhalifu wowote niko tayari kwenda na nitarejea,” alisema Rais Kiir wakati wa mahojiano na Kituo cha Televisheni cha Citizen.Alisema yeye si kikwazo cha amani huku akiamini mkataba wa amani kati ya serikali na makundi ya upinzani hautavunjika… “nina uhakika na ninawahakikishia wananchi kuwa nchi itakuwa na amani,” alisema.Rais Kiir alikubali kuna maofisa wa serikali waliohusika na utakatishaji fedha za nchi hiyo na kuacha wananchi wengi wakisumbuka katika umasikini, lakini kwa sasa amejikita kuleta amani kabla ya kuchukua hatua kwa wahusika wote.
2
MIUNDOMBINU ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam awamu ya pili hadi ya nne, imetengewa Sh bilioni 28.79 katika mwaka wa fedha 2019/2020.Awamu ya pili itahusisha barabara ya Kilwa kutoka katikati ya jiji hadi Mbagala; Chang’ombe kutoka makutano ya barabara ya Kilwa/ Chang’ombe hadi makutano ya barabara ya Nyerere/ Chang’ombe, Kawawa kutoka kutoka makutano ya barabara ya Nyerere/ Kawawa hadi makutano ya barabara ya Morogoro/ Kawawa na Sokoine Drive.Akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe alisema barabara hizo zina urefu wa kilometa 20.3. Kazi nyingine zitakazofanywa ni ujenzi wa flyovers mbili katika makutano ya barabara za Mandela/Kilwa na Nyerere/Kawawa na ujenzi wa vituo. Kamwelwe alisema kuhusu awamu ya tatu na ya nne ya BRT, kazi zitakazofanywa ni kuendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara zilizopo kwenye awamu hizo.Barabara hizo ni Uhuru, Nyerere, Bibi Titi na Azikiwe zenye urefu wa kilometa 23.6. Awamu ya nne nne yenye urefu wa kilometa 25.9 itahusisha ujenzi wa barabara ya kupitia Ali Hassan Mwinyi hadi Morocco na kuendelea hadi Tegeta kupitia Mwenge.Vile vile itahusisha Barabara ya Sam Nujoma na kuungana na mradi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka awamu ya kwanza katika Kituo Kikuu cha Ubungo. Kamwelwe alisema katika mwaka wa fedha 2019/2020 kazi zitakazofanyika ni mapitio ya usanifu na ujenzi mradi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka awamu ya tatu na usanifu wa kina na ujenzi wa awamu ya nne.Aidha, awamu ya tano na sita ya mradi wa miundombinu hiyo zitafanyiwa usanifu wa kina. Kuhusu Mfuko wa Barabara alisema unatarajia kwa mwaka wa fedha 2019/2020 kukusanya jumla ya Sh 839,127,000,000 zitakazotumika kufanya kazi za matengenezo ya barabara nchini.
3
WAANDISHI WETU – DAR/MIKOANI KASI ya virusi vya ugonjwa wa corona inazidi kuenea huku Watanzania wakitakiwa kuendelea kuchukua tahadhari kama njia ya kuepuka maambukizi hayo. Jana Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitangaza ongezeko la wagonjwa wa corona baada ya watu wengine wawili kuthibitishwa Visiwani Zanzibar na Dar es Salaam ambao  wote ni raia wa kigeni. Hiyo inakuja siku moja baada ya juzi kutangaza kufungwa kwa shule zote kwa siku 30 ikiwa ni hatua ya kuzuia kuenea kwa maambukizi ya corona nchini. Serikali imethibitisha hayo baada ya wagonjwa hao wawili kufanyiwa vipimo vya maabara katika Maabara Kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii. Alisema sampuli ya kwanza ni ya mwanaume, raia wa Marekani, 61 ambaye ni mkazi wa Dar es Salaam. Mgonjwa huyo ametengwa katika sehemu maalumu kwa taratibu nyingine za kitabibu, pia ufuatiliaji wa watu waliokuwa karibu naye. Zanzibar kwa upande wake imesema sampuli ya pili iliyopokelewa ni ya mwanaume mwenye umri wa miaka 24, raia wa Ujerumani.       WATU 27 WASUBIRI VIPIMO Kutokana na kile kinachoonekana kuendelea kudhibiti maambukizi hayo ya corona, Serikali imesema kuwa sampuli za watu 27 wanaodaiwa kushirikiana kwa namna moja ama nyingine na mgonjwa wa kwanza wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona, Isabela Mwampamba (46), zimetumwa Maabara Kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii, Dar es Salaam. Majibu ya sampuli hizo yanatarajiwa kutolewa wakati wowote kuanzia sasa. Isabela ambaye ni mmiliki wa shule binafsi ya Upendo Friends iliyopo jijini Arusha, anaendelea na matibabu katika eneo maalumu. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini hapa, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu,  alisema hadi sasa katika Mkoa wa Arusha, watu hao 27 wakiwemo waliokuwamo katika hoteli aliyofikia Isabela wako chini ya uangalizi maalumu. “Kwa upande wa Arusha sasa hivi tunafuatilia watu 27 ambapo leo (jana) wako siku ya tatu na maendeleo yao ni mazuri, hivyo kuanzia sasa wakati wowote majibu ya sampuli yatatolewa,” alisema Ummy. IDADI YA WAGONJWA Alisema hadi kufikia jana wamethibitisha uwepo wa virusi hivyo kwa wagonjwa wawili baada ya kufanyiwa vipimo vya maaabara katika Maabara Kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii Dar es Salaam. “Sampuli ya kwanza ni  hiyo mwanaume raia wa Marekani (61), mkazi wa jijini Dar es Salaam na amewekwa mahali maalumu kwa ajili ya taratibu nyingine za kimatibabu ikiwemo  kufanya ufuatiliaji wa watu waliokuwa karibu naye. “Baada ya kushauriana na Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hamad Rashid, napenda kutangaza sampuli ya pili iliyofanyiwa vipimo na kuthibitisha uwepo wa virusi hivyo iliyopokelewa kutoka Zanzibar ni ya mwanaume (24) ambaye ni raia wa Ujerumani. “Muhimu kila mmoja wetu kuzingatia maelekezo ya kujikinga ugonjwa huu yanatolewa mara kwa mara, hivyo kwa sasa tuna wagonjwa watatu wenye maambukizi ya virusi hivyo,” alisema Ummy. Hata hivyo taarifa ya Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid ilisema mgonjwa huyo ni raia wa Ghana aliyeingia Zanzibar akitokea Ujerumani.  MAABARA KUWA MOJA Ummy alisema tangu wametangaza kisa cha kwanza cha mgonjwa wa corona nchini, kumekuwa na maswali kwanini sampuli zote zinapelekwa Maabara ya Taifa, Dar es Salaam. “Ufafanuzi ni kwamba kirusi hiki kinapimwa katika maabara maalum ambapo kuna ngazi, kwa nchini ni maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii tu ambayo iko ngazi ya tatu katika upimaji wa sampuli wa virusi ambavyo vina hatari ya kuambukiza kwa kiasi kikubwa “Kama mlikuwa mnafuatilia kabla ya Februari 15, barani Afrika, Kusini mwa Sahara, ilikuwa na maabara mbili tu ambazo zilikuwa na uwezo wa kupima kirusi hiki cha corona, maabara ya Afrika Kusini na Senegal. “Hata sisi tumefanya kazi kubwa ya kuhakikisha maabara yetu inakuwa na uwezo wa kupima sampuli, kupitia jukwaa hili niwatoe wasiwasi Watanzania tuliweka mipango sampuli ikichukuliwa inasafirishwa vipi, tumeshasaini mikataba pia jinsi ya kusafirisha sampuli,” alisema Ummy. Alisema hata wakati wa tishio la ebola, sampuli zote zilikuwa zinapelekwa Dar es Salaam na kuwa katika mlipuko wa corona kuna vipimo vya kupima haraka – ‘rapid test’, ambavyo ni vya awali na wameshaandaa utaratibu wa kuhakikisha wanavipata kwa haraka ili kusambaza katika maabara za ngazi ya mikoa. VITUO VYA AFYA Ummy amevitaka vituo vyote vinavyotoa huduma za afya hususani binafsi kuhakikisha wanapokuwa na mshukiwa watoe taarifa kwa mamlaka husika na kila mkoa kuna timu ya dharura. “Tumeona kwa Dar es Salaam kila mgonjwa anaambiwa nenda Muhimbili akiwa na mafua. Kuna kitu kinaitwa ‘standard case definition’, siyo kila mwenye mafua, homa au kikohozi basi ni mshukiwa wa corona, hiyo inasababisha kutoa mzigo kwa mfumo mzima wa utoaji huduma za afya.  “Vituo vya Serikali na binafsi vizingatie miongozo iliyotolewa na wizara kuhusu hatua za kupeleka wagonjwa wanaoshukiwa kuwa na virusi vya corona,” alisema Ummy.  MGONJWA AOMBA RADHI Akizungumzia hali ya mgonjwa wa kwanza, Isabela, Waziri Ummy alisema anaendelea vizuri na kuwa aliwasiliana naye asubuhi hana kifua, kikohozi, wala homa na amekuwa akijipima homa mara tatu kwa siku.  “Sasa hivi Isabela anaendelea vizuri na yupo tayari kutoa elimu na taarifa zaidi kwa wananchi juu ya kujikinga kwani tumeona watu wameanza ku-panic na kuwa na hofu na kutoa taarifa nyingi za uongo ambazo hazijathibitishwa,” alisema Ummy. Aidha alilazimika kumpigia simu Isabela ambaye aliridhia kuwekwa ‘Live’ katika mkutano na wanahabari na aliomba radhi kutokana na kuwa mgonjwa wa kwanza na kuzua taharuki kubwa nchini. “Nashukuru sana waandishi wa habari na Watanzania wote kwa ujumla, naendelea vizuri. Cha kwanza namshukuru Mungu kwa kunilinda na wananihudumia vizuri. “Lakini pia nawashukuru Watanzania, ninatamani kusema kwamba ninawaomba msamaha kwa maana kwamba ya kuwa mgonjwa wa kwanza wa corona Tanzania imeleta taharuki nchi nzima na watu wengi wameona kwamba mimi ni kisababishi, niko hapa kuomba msamaha mkubwa. “Ni jambo limeshatokea, mimi naamini Mungu ataendelea kutuponya. Natamani nitoe ujumbe huu kwa Watanzania tutumie wakati huu kuelimishana ugonjwa ukoje na siyo kukuza jambo kwani ni ugonjwa uko duniani kote, kwani hofu ni kubwa zaidi ya corona,” alisema Isabela. KITENGO MAGONJWA YA MLIPUKO Awali Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Udhibiti na Ufuatiliaji wa Magonjwa ya Milipuko, Dk. Janneth Mghamba, alisema timu ya taifa iliwasili mkoani Arusha  kushirikiana na mkoa huo kufanya ufuatiliaji kwa mgonjwa wa kwanza. Alisema kwa sasa wanafuatilia watu hao 27 waliokuwa naye karibu na wamefanya mawasiliano na wanaendelea vizuri na wataendelea kuwepo mkoani Arusha ili kuweka mikakati ugonjwa usisambae zaidi. “Mgonjwa anaendelea vizuri sana, hana homa kwa sababu dalili kubwa tunazoangalia ni homa, kukohoa na kubanwa na mbavu na tumechukua sampuli za waliokuwa karibu naye na mrejesho tutatoa tukimaliza,” alisema Dk. Mghamba. Akizungumzia matumizi ya kujikinga vikiwemo vitakasa mikono (sanitizer) na vile vya kuziba pua na mdomo, alisema vifaa hivyo vinatakiwa kuvaliwa maeneo yenye msongamano wa watu badala ya kuvaliwa kama vinavyovaliwa sasa na baadhi ya watu. “Mask zinavaliwa na tafiti zimeonyesha inavaliwa na mtu mwenye maambukizi kusudi asimwambukize mwingine, ila pia zinaweza kuvaliwa kwenye maeneo yenye msongamano.  “Lakini kwa sababu Serikali imepiga marufuku msongamano, hatutegemei kukuona wewe unavaa mask unapita sehemu ambayo hakuna msongamano,” alisema Dk. Mghamba. ATHARI ZA MASK Akizungumzia athari za mask, Dk. Mghamba alisema kuwa inaweza kuwa kubwa kwani watu wegi bado hawajui kama zinatakiwa kubadilishwa kila baada ya saa nne. “Ukikaa nayo siku nzima ni hatari, inaweza kukuletea athari zaidi,” alisema Dk. Mghamba. MUFTI AFUNGA MADRASA Katika kile kinachoonekana kuchukua tahadhari na kudhibiti kasi ya maambukizi ya corona, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir, amewataka walimu wa madrasa  zote nchini  kuzifunga ili kuepusha kuenea kwa virusi  hivyo. Pamoja na hali hiyo amewataka Waislamu waliopo kwenye maeneo yanayoshukiwa  kuwa na wagonjwa wa corona kutohudhuria swala ya Ijumaa na swala zote za jamaa kwa kuwa ni haramu. Alisema uamuzi huo umefikiwa na kikao cha dharura kilichoketi wiki hii cha Baraza la Ulamaa la Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) ambacho kilijadili mwenendo wa ugonjwa huo na tabia zake. Mufti alisema uamuzi wa kufunga madrasa kunatokana pia na agizo la Serikali la kusitisha masomo kwa shule zote kuanzia ngazi za awali hadi vyuo vikuu. “Tunawaomba waumini wote wa Kiislamu kutekeleza agizo hili kwa lengo la kuokoa nafsi zetu zisiangamie, ni ibada kubwa na mtekelezaji wa amri na maagizo haya atalipwa  thawabu zisizo na kifani,” alisema Mufti Zubeir. Alisema mamlaka zinazohusika zikitangaza karantini kwa eneo lolote, Waislamu wa eneo hilo wanaruhusiwa na sheria ya Kiislamu kutohudhuria swala ya Ijumaa na swala zote kwani lengo la swala ni kujenga umoja, pia kuleta masilahi na manufaa kwa waumini. Alisema Muislamu yeyote atakayepatwa na maradhi hayo ni haramu kwake kuhudhuria swala ya Ijumaa na swala za jamaa kama ambavyo ni haramu kwake kuchanganyika na watu wengine kwani kufanya hivyo ni kuisambaza na kueneza ugonjwa huo kwa wenzake. MPAKA WA NAMANGA Aidha Waziri Ummy alifanya ukaguzi eneo la mpaka wa Tanzania na Kenya wa Namanga ambako aliagiza wataalamu wa afya mipakani kote nchini kuwa makini katika kufanya ukaguzi kwa wasafiri wanaopita. Alisema moja ya dalili kubwa ya magonjwa ya corona ni pamoja na homa kali, hivyo ndiyo maana kipimo hicho hufanyika ila ni muhimu zaidi kuhoji wasafiri kabla ya kuwaruhusu kupita ili kubaini historia ya maeneo waliyotoka. “Maofisa afya mipakani tunatakiwa tuweke umakini zaidi katika ukaguzi wa wasafiri na watu wanaopita katika maeneo yetu, siyo kuangalia joto la mwili tu. Jana nilikuwa naangalia China, kuna mtu amemeza vidonge vya kushusha homa kusudi aweze kupita, maofisa afya ni wajibu wenu kufanya uchunguzi zaidi,” alisema Ummy. JET YAFUNGA OFISI Kutokana na athari ya maambukizi ya virusi vya corona, jana uongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET) ulitangaza kufunga kwa muda ofisi na badala yake wafanyakazi watafanya shughuli zao wakiwa nyumbani. Taarifa iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa JET, Dk. Ellen Otaru, ilieleza kuwa chama hicho kina  wajibu wa kujikinga na kukinga watu wanaowazunguka pamoja na mazingira.  “Hivyo basi, tunaomba wanachama wetu mfanye kazi kwa usalama na kwenye mazingira salama. Uongozi umeamua kusitisha kazi/shughuli zote ofisini kuanzia leo, na ofisi itafungwa kwa kipindi kisichopungua wiki tatu. Tutawajulisha kadiri taarifa zitakavyokuwa zinapatikana.  “Kuna taarifa nyingi zinarushwa kwenye mitandao ya jamii kuhusu Covid-19. Sio dalili zote zitaonekana, na ndio maana tuchukue tahadhari kama ifuatavyo: Osha mikono pamoja na koki ya bomba kila wakati kwa sabuni ya maji na maji safi na salama. Usishike koki, kishikio cha mlango, baada ya kunawa mikono, tumia karatasi, kisha itupe. “Osha vyombo kwa maji na sabuni, hasa vijiko, vikombe, glasi. Mjitahidi mkiwa kazini kwenye kutafuta habari kuvaa mask, na msiazimane. Ukirudi nyumbani, vua nguo bafuni na uoge kabla hujakaa na familia yako. “Kama huna sanitizer, tumia kilevi kama whisky, K-Vant, Konyagi n.k kufuta mikono, kalamu, miwani, compyuta. Tumia vifaa vya kazi vyako binafsi na usiazime kwa mtu au kutoka kwa mtu.  “Iwapo utajisikia uchovu, maumivu kidogo kama malaria, pima uhakiki sio malaria. Kisha kaa nyumbani mara moja na unywe maji kwa wingi kila mara, ili kirusi kishuke na kisiingie kwenye mapafu,” alisema Dk. Ellen. TMDA YATOA ELIMU Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imetoa mafunzo maalumu kwa watumishi wake ya kupambana na kuzuia corona. Mafunzo hayo yalitolewa na Ofisa Majaribio na Usalama wa dawa wa mamlaka hiyo, Dk. Alex Nkayamba katika ofisi za TMDA zilizopo Dar es Salaam. Dk. Nkayamba alieleza kuwa watumishi hao kutoka idara mbalimbali za mamlaka hiyo waliweza kupokea mafunzo na watakuwa mfano na walimu kwa wengine katika maeneo ya kazi na nyumbani. “Hadi sasa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza uwapo wa visa vitatu vya wagonjwa wa corona, ugonjwa huo umekuwa ukienea kwa kasi karibu nchi mbalimbali duniani ambapo tayari mamlaka zimewataka wananchi kuchukua hatua mahsusi za  kujikinga na kuondoa hofu. “Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuziba mdomo wakati wa kukohoa, kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka mara kwa mara ama kwa vitakasa mikono (hand sanitizer) pamoja na kuepuka sehemu zenye mikusanyiko ya watu,” alisema Dk. Nkyamba. MOROGORO YAJIPANGA Serikali mkoani Morogoro imetenga moja ya wodi katika Hospitali ya Wilaya ya Morogoro iliyopo Mkundi kuwaweka  karantini wagonjwa wa corona pindi watakapohisi kukumbwa na ugonjwa huo. Hayo yalibainishwa jana kwenye kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi Manispaa ya Morogoro kilichowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo watendaji wa halmashauri, viongozi wa dini, watu maarufu, wafanyabiashara na wanahabari. Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo alisema tahadhari hiyo imechukuliwa na manispaa kuhakikisha wananchi hawapati maambukizi hayo. Aliagiza kituo kikuu cha mabasi Msamvu, viwandani, hospitali, vituo vya mabasi na kwenye usafiri wa jumuiya kuwekwa huduma ya maji ya kunawa sambamba na kuhakikisha usafi unafanywa kwenye maeneo husika. HABARI HII IMEANDALIWA NA JANETH MUSHI (ARUSHA), CHRISTINA GAULUHANGA,  AVELINE KITOMARY (DAR ES SALAAM) NA ASHURA KAZINJA (MOROGORO)
3
Na Fredy Azzah, Dodoma Uchache wa wabunge waliohudhuria Mkutano wa 11 ulioanza leo mjini Dodoma, umemtisha Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM), ambapo amehoji endapo kiapo cha wabunge wapya wa Chama Cha Mapinduzi Dk. Godwin Mollel (Siha) na Mauld Mtulia (Kinondoni) walioapishwa leo ni halali ama la. Leo wakati wabunge hao wakila kiapo cha uaminifu mbele ya Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson, wabunge wa upinzani waliokuwamo bungeni ni takribani wanne tu wa Chama cha Wananchi (CUF). Mlinga amehoji hayo baada ya kipindi cha maswali na majibu, Mlinga akiomba mwongozo wa Spika, kama kiapo cha wabunge hao ni halali kwa sababu wameapa huku wabunge wakiwa nusu idadi yao. Aidha, amehoji pia endapo wabunge walioudhuria bunge hilo watalipwa posho kwa sababu ya akidi kutotimia na ni hatua gani zitachukuliwa kwa wale ambao hawakuhudhuria. Akijibu mwongozo huo, Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia amesema: “Mlinga kauliza kuhusu akidi, kwa sababu anasema kikanuni inatakiwa wabunge wawe nusu, lakini kanuni ya 77 (1-5), inasema kuhusu shughuli za uendeshaji wa Bunge na akidi. “Akisema akidi haijatimia sijui yeye ndiyo kahesabu hao wabunge ama vipi, niseme tu suala la akidi ni wakati wa kuanza kikao kwa hiyo mwongozo anaoutaka sasa haupo kikanuni, kwa hiyo walioapishwa wameapishwa kihalali”. Pamoja na wabunge hao wanne wa CUF, walikuwapo wabunge wawili wa Chadema ambao ni Serengeti, Chacha Marwa na Joyce Sokombi wa Viti Maalumu. Hadi kipindi cha maswali na majibu kinakwisha, wabunge wa upinzani walikuwa 18 huku pia wa CCM wakiwa takribani nusu ya idadi yao. Idadi hiyo iliendelea kubaki hivyo hadi Bunge linaahirishwa saa saba mchana huku mawaziri na manaibu waziri waliokuwa wameketi kwenye viti vyao walikuwa chini ya 10.
3
Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani imesema ina maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda na hoteli hivyo watu waende kuwekeza.Imesema, kuna eneo kubwa la uwekezaji la EPZ (ukanda wa kiuchumi) lililotengwa kwa ajili ya viwanda na maeneo ya watu yanayopatikana kwa kuzingatia taratibu za kisheria.“Watu wakifika pale EPZ kwa Mkurugenzi wa EPZ wanaweza wakapata maelekezo mazuri ya uwekezaji hasa kwenye uzalishaji wa viwanda vikubwa ambavyo vitauza bidhaa ndani na nje ya nchi” amesema Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Fatuma Latu.Amesema, halmashauri hiyo pia imetenga maeneo kwa ajili ya viwanja vya ndege na kwa sababu ya kasi ya ujenzi wa viwanda yataboreshwa.Latu amesema, Bagamoyo ina barabara nzuri hivyo mwekezaji au mteja anaweza kulala hapo na asubuhi akawahi kikao Dar es Salaam au akalala Dar es Salaam na akafanya kazi Bagamoyo.“Lakini pia mtu anaweza akatoka Dar es Salaam akaja akapumzika Bagamoyo halafu baadaye akaendelea na safari yake” amesema ofisini kwake wakati akizungumza na timu ya wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN).Wafanyakazi wa TSN wapo Bagamoyo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maonesho ya Viwanda Mkoa wa Pwani 2019 na Kongamano la Fursa za Biashara na Uwekezaji mkoani humo.“Unaweza ukaenda mpaka Msata unaenda Morogoro, lakini pia tunatoka kwenda Tanga, kwenda Moshi na Arusha. Kwa hiyo sehemu ambayo unaiona ni nzuri yaani kama njia panda ya kwenda kila mahali panafikika”amesema Latu.Amesema, wanajivunia kuna na mambo na vitu vinavyoweza kuvutia watu kwenda kuwekeza ikiwa ni pamoja rasilimali ardhi, amani na utulivu, na uwepo wa maeneo ya kihistoria ikiwa ni pamoja na Mji Mkongwe.Kwa mujibu wa kiongozi huyo, kwa sasa halmashauri ina viwanda vikubwa, vidogo na vya kati, na kwamba, sera ya Tanzania ya Viwanda imehamasisha wadau hivyo kuna ujenzi unaoendelea.“Viwanda vipo, wawekezaji ambao wapo nje karibuni sana Bagamoyo kuwekeza, Bagamoyo ni shwari, ipo salama” amesema.
5
Na BRIGHITER MASAKI MSANII wa Filamu nchini, Elizabeth Michael (Lulu), amesema yupo katika maombi ili aweze kuolewa kama alivyopanga. Lulu alisema hayo alipokuwa kwenye sherehe za harusi ya msanii wa muziki wa Bongo Fleva na Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule (Profesa Jay), iliyofanyika juzi kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. “Namuomba Mungu anipiganie kwenye uhusiano wangu ili niweze kutimiza lengo langu la ndoa na mtu niliyenaye kwenye uhusiano wa kimapenzi. “Ndoa ni jambo la kutokea kati ya makubaliano yetu hivyo siku nikiolewa nitakachotoa kama zawadi kwa mashabiki wangu ni uhuru wa kuniuliza chochote watakacho na nitawajibu,” alieleza Lulu aliyekuwa amevalia vyema gauni lake. Licha ya kueleza hayo Lulu hakuwa tayari kumtaja wala kumzungumzia mpenzi wake wa sasa. “Sipo tayari kuzungumzia kitu kinachohusu mahusiano yangu kwa sasa, tukijijua wenyewe inatosha, wengine watajua mpaka siku ya ndoa yangu ambapo nitajibu na kuzungumzia mambo yote mnayotaka kujua kuhusiana na uhusiano wangu maana vitu vya ndoa vinakujaga tu, namuomba Mungu azidi kunipigania na kunipangia malengo yangu ya ndoa na kuwa na familia yatimie,” alisema Lulu.
1
TAASISI ya Kuzuia na Kapambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Ruvuma imemfi kisha katika Mahakama ya Wilaya ya Mbinga Ofisa Mtendaji wa Kata ya Linda, Cosmas Nyoni akituhumiwa na makosa ya kuomba na kupokea fedha kwa njia ya rushwa.Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Ruvuma, Owen Jasson, mshitakiwa amefanya kosa kinyume cha kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007.Jasson alidai Agosti 3, 2018, Ofisi ya Takukuru Wilaya ya Mbinga ilipokea taarifa kuwa Nyoni kwa njia za rushwa Juni 29, 2018 aliomba Sh 550,000 kutoka kwa Zacharia Komba ili asimchukulie hatua na kumpelekea watu wa upekuzi nyumbani kwake ili kumpekua kwa makosa ya kujihusisha na ununuzi holela wa kahawa iliyopigwa marufuku ya magoma.“Siku hiyo mtuhumiwa alipokea fedha kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ni sehemu ya fedha alizoomba na siku ya Julai 4, 2018 alipokea tena fedha nyingine kiasi cha shilingi 250,000, pia ikiwa ni sehemu ya fedha alizokuwa ameomba,” alidai Jasson.Alidai baada ya kupokea taarifa hiyo, uchunguzi ulifanyika ambao ilithibitika kwamba ni kweli mshitakiwa alitenda makosa ya rushwa, hivyo Mei 17, mwaka huu, amefikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mbinga na kufunguliwa kesi ya jinai namba 41 ya mwaka 2019.Kulingana na Naibu Mkuu wa Takukuru, kesi hiyo imesomwa na Wakili wa Serikali, Chali Kadeghe mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbinga, Aziza Mbadjo.
3
Na CHRISTOPHER MSEKENA MUZIKI wa Bongo Fleva umempokea kwa mikono miwili mwanamitindo Hamisa Mobetto baada ya kuachia ngoma yake ya kwanza Madam Hero, iliyoweka rekodi ambayo baadhi ya wanamuziki nchini wameshindwa kuifikia. Wimbo huo ulioandikwa na mtunzi Foby na kutengenezwa na Prodyuza C9 Kanjenje, umelenga kumpa hamasa ya kutokata tamaa mwanamke katika kupambana kwa kufanya shughuli mbalimbali za kujikwamua kimaendeleo bila kurudishwa nyuma na changamoto zilizopo katika jamii. Mwanamitindo huyo ambaye pia ni mwigizaji amejiwekea rekodi ambayo wana Bongo Fleva wengi huwa wanashindwa kuifikisha ya wimbo wake Madam Hero, kusikilizwa na watu zaidi ya  200,000 ndani ya siku moja katika mtandao wa Youube. Hatua hiyo imemfanya Mobetto awe gumzo kila kona kutokana na wimbo wake kupokelewa vizuri siyo na mashabiki pekee bali mastaa mbalimbali wamejitokeza kumpongeza  kwa kutoa ngoma hiyo huku wengine kuibuka na kumponda wakidai hawezi kuimba na siyo kila mtu anaweza kuwa msanii. Hamisa amewatumia wanawake wenye mafanikio barani Afrika kama vile Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu, staa wa filamu nchini Marekani akitokea Kenya, Lupita Nyong’o, Mama wa Afrika na msanii wa muziki, Yvonne Chaka Chaka na Miriam Makeba. Swaggaz tumeona tukupe orodha ya warembo ambao muziki kwao haukuwa chaguo la kwanza kama vile anavyofanya Hamisa lakini walipojaribu wakafanikiwa, hadi leo hii ni mastaa wakubwa wa muziki Bongo. LULU DIVA Lulu Abbas maarufu katika anga la Bongo Fleva kwa jina la Lulu Diva, mrembo ambaye tulianza kumwona katika vichupa vya wasanii kama ‘Video Vixen’ miaka miwili iliyopita lakini sasa hivi ni staa mkubwa wa muziki akisimamiwa ya Lebo ya Born To Shine AR. Lulu Diva ambaye hakuaminiwa sana alipoanza kuimba, anasema Hamisa ni mtu anayempa hamasa katika mambo mbalimbali na tayari wana kolabo ambayo wakiitoa itasumbua chati za muziki Bongo. “Mobetto ni mfano wa kuigwa na wanawake wengi, amekuwa akijaribu kufanya vitu vingi na kufanikiwa, kuna kitu chetu tunakiandaa yaani sijui tukikitoa itakuwaje,” alisema Diva alipochonga na Swaggaz. VANESSA MDEE Hakuna anayeweza kubisha kwamba ndiyo msanii namba moja wa kike mwenye mafanikio kwa sasa, amefanikiwa kimuziki licha ya safari yake kuanzia kwenye tasnia ya habari akiwa kama mtangazaji. Ukimtazama Vee Money, alipotoka mpaka alipo sasa hivi unaweza kukosa sababu ya kumchukulia poa mwanamitindo Mobetto katika safari yake mpya kwenye muziki. SHILOLE Zuwena Mohamed ‘Shilole’ yupo kwenye orodha ya wasanii watano wa kike wenye thamani kubwa Bongo, lakini muziki aliuanza kama masihara lakini alipowekeza nguvu akaacha kuigiza na kujikita rasmi muziki. Hamisa anakanyaga nyayo za Shilole kwa sababu wimbo wake Madam Hero, umetengenezwa na mikono ya C 9 Kanjenje, prodyuza aliyetengeneza wimbo wa kwanza wa Shishi aliomshirikisha Q Chief, Lawama uliotoka miaka sita iliyopita. GIGY MONEY Huyu ni mrembo mwingine ambaye anachukia sana kwa sasa ukimtambua kama Video Vixen, anataka afahamike kama msanii wa muziki kwani ngoma zake kama Nampa Papa, Mimina, Kiki ni Gigy na nyinginezo zimemfanya apate shoo kibao kama mwanamuziki. AMBER LULU Muziki haukuwa chaguo la kwanza kwa Amber Lulu, tulimfahamu kama mrembo anayependezesha video za muziki lakini alipoingia kwa miguu miwili kwenye muziki sasa hivi hakamatiki kwenye Bongo Fleva. Amber Lulu, anasema sasa hivi ameamua kuacha matukio yote mabaya na skendo zilizomchafua ili ajikite kwenye muziki kwa sababu sasa hivi ameufanya kama kazi yake ya kudumu. Hivyo basi ukiwatazama warembo hao wa Bongo, unaweza kuona kuwa Hamisa, anaweza kuja kuwa msanii wa muziki mpaka watu wakaanza kusahau kama ni mwanamitindo kama ataufanya muziki kwa kumaanisha kwani uwezo tayari ameonyesha na mashabiki wamempokea. Muda utaongea.
1
Na ASHA BANI-DAR ES SALAAM KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amefanya ziara kimya kimya jijini Dar es Salaam, kwa kutembelea wagonjwa na kutoa pole kwa wafiwa wa chama hicho. Ziara hiyo aliifanya jana huku akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wa chama hicho akiwamo Mbunge wa Temeke, Abdalah Mtolea (CUF), Naibu Meya wa Jiji, Mussa Kafana na Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omar Kumbilamoto. Katibu mkuu huyo alifanya ziara hiyo katika kata za Gongolamboto, Majohe, Kigamboni na Upanga, ambapo alizungumza na wananchi mbalimbali aliowakuta katika maeneo husika kwa kuwataka kuwa watulivu, huku akiahidi changamoto zinazokikabili chama hicho zitamalizika hivi karibuni. Mbali na hilo pia aliwaahidi wanachama wa chama hicho kujiandaa kuchukua ofisi yao Buguruni muda wowote kuanzia sasa kwani wamefikia katika hatua nzuri. Akizungumza na MTANZANIA jana Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari Mahusiano na Umma, Mbarara Maharagande, alisema ziara ya kukagua uhai wa chama na kufungua matawi jijini Dar es Salaam ipo kama ilivyopangwa na tarehe husika itatangazwa kwa umma. “Hii ni ziara ya kawaida na inalengo la kuwatembelea wanachama wetu ambao walipatwa na matatizo mbalimbali ikiwemo maradhi na hata wengine kufiwa. Kwa hiyo Katibu Mkuu alikwenda kuwapa mkono wa pole jambo ambalo ni kawaida kwa binadamu yeyote na kama unavyofahamu Maalim Seif ni kiongozi wa watu na siku zote amekuwa akiishi uungwana huo,” alisema Maharagande. Ziara hiyo ya kimya kimya imekuja siku chache baada ya Jeshi la Polisi kuzuia wanachama wa chama hicho, waliokuwa wamehamasishwa na Mbunge wa Temeke kwenda kufanya usafi katika ofisi za CUF Buguruni, Aprili 30, mwaka huu. Hata hivyo, Jeshi la Polisi lilimzuia kwa Maalim Seif na wafuasi wake kufanya hivyo kwa maana ya kuweza kuhatarisha amani kwa wananchi iliyopo. Juzi waaliodaiwa wafuasi wa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba walimdhibiti mtu mmoja ambaye walidai ni wa upande wa Maalim Seif aliyefika katika ofisi hiyo kwa ajili ya kufanya usafi. “Sisi tulishazuiwa kufanya hivyo na tulikuwa tunajipanga kwa ajili ya kufanya ziara katika tarehe nyingine hao waliofika katika eneo hilo watakuwa wametumwa na wametengenezwa ,” alisema Maharagande. Hivi karibuni wafuasi wa Profesa Lipumba walivamia Hotel ya Vina iliyopo Mabibo Wilaya ya Ubungo na kuzua vurugu zilizosababisha waandishi wa habari kupigwa.
3
AWAMU ya pili ya ujenzi wa reli ya kisasa kwa kiwango cha kimataifa kwa kipande cha Morogoro - Makutupora, imeanza kwa kasi huku nguvu ikielekezwa katika sehemu korofi , hasa zenye athari za mara kwa mara nyakati za mvua katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Morogoro na Dodoma.Mkoani Morogoro, maeneo korofi yapo zaidi wilayani Kilosa katika Mto Mkondoa unaoathiri miundombinu, makazi na hata mashamba ya watu, wakati kwa upande wa Dodoma, athari za mara kwa mara katika eneo la Gulwe, wilayani Mpwapwa.Umbali kati ya maeneo hayo `sugu’ mawili ni takribani kilometa 83. Akizungumza wakati wa ukaguzi wa awamu ya pili ya mradi huo jana, Meneja wa Mradi wa reli ya kisasa ya SGR kwa kipande cha Morogoro-Makutupora, Faustine Kataraia alisema kutokana na jiografia ya maeneo hayo, maeneo yenye milima yatachongwa, mengine kutengenezwa mahandaki ili kuruhusu reli kupita ndani ya milima kwa umbali wa takribani kilometa moja.“Kama hapa Kilosa, athari za Mto Mkondoa zinafahamika na mara nyingi ziliharibu miundombinu ya reli kiasi cha kufanya nyakati za mvua safari ziahirishwe mara kwa mara. “Sasa, kwa mradi huu mpya na wa kimataifa wa reli ya kisasa ya SGR, athari za mafuriko zitabaki kuwa historia kwani reli zitapitishwa mbali na Mto Mkondoa ambao ni moja ya sehemu korofi sana, ni eneo kama la kilometa 83 kati ya Kilosa na Gulwe, wilayani Mpwapwa.“Hivyo njia ya reli itahamia milimani na hii inamaanisha kwamba tutakuwa na madaraja makubwa, ya kawaida, makalavati, lakini pia tutakuwa na tunnels (mahandaki) kama nne. Hizi tunnels zitakazokuwepo zitakuwa na urefu wa jumla ya kilometa 2.7, lakini refu zaidi litakuwa na takribani meta zaidi ya 800 hadi 900, yaani karibu kilometa moja, hii itatobolewa chini ya mlima na kuibukia katika daraja la juu linalopita katika mto Mkondoa kwa umbali wa kilometa moja na kuingia tena katika mlima mwingine,” alisema.Mhandisi huyo mkongwe alisema tayari kazi za kuchoronga milima hiyo na usanifu mwingine zinaendelea. Kazi nyingine zinazoendelea katika mradi huo uliofikia asilimia 4.5 tangu ukabidhiwe kwa mkandarasi, kampuni ya Yapi Merkezi ya Uturuki Februari mwaka huu, ni pamoja na kusafisha eneo la ujenzi, kukata udongo usiohitajika na kujaza vifusi, uthamini wa maeneo yatakayopisha mradi na kadhalika.Aidha, mkandarasi ambaye pia anafanya kazi hiyo katika kipande cha Dar es Salaam- Morogoro kilichokamilika kwa zaidi ya asilimia 36, ikiwa ni pamoja na kutandaza mataruma na reli, anaendelea kuongeza vifaa vya kazi na wafanyakazi katika mradi wa awamu ya pili unaotarajiwa kukamilika ndani ya miezi 36 kuanzia Februari mwaka huu.Mitambo ya kusaga mawe kwa ajili ya kokoto imeshafungwa katika eneo la Kimambila, wilayani Mvomero na ina uwezo wa kuzalisha tani 300 za kokoto kwa saa. Dhamira ya mkandarasi ya kufanya kazi usiku na mchana ili zipatikane tani 6,000 kila siku. “Pia kwa sababu reli yetu itatumia umeme, unafanyika ujenzi wa njia maalumu ya umeme kwa ajili ya mradi.Upande wa Morogoro – Makutupora kutakuwa na vituo saba vya kupozea umeme utakaopozwa kutoka Kilovoti 220 hadi kilovoti 25,” alisema Kataraia. Kati ya Morogoro na Makutupora kunatarajiwa kuwa na stesheni za Mkata, Kilosa, Kidete, Igandu, Dodoma Mjini, Bahi na Makutupora. Awamu ya pili ya mradi itakuwa na jumla ya kilometa 336 za njia kuu na kilometa 86 za njia ya kupishania treni, jumla yote ni kilometa 422.Hizi zikiunganishwa na jumla kilometa 300 za awamu ya kwanza kati ya Dar es Salaam na Morogoro, awamu hizi mbili zitakuwa na jumla ya kilometa 722. Mradi huo uliogawanywa katika vipande vitano, hadi kukamilika unatarajiwa kuwa wa kilometa 1,219 kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza. kipande cha kwanza ni kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kitakachogharimu Sh trilioni 2.7.“Kipande kingine ni kutoka Morogoro hadi Makutupora chenye urefu wa kilometa 422 ambacho kitagharimu Sh trilioni 4.4, Makutupora hadi Tabora kilometa 376.5, Tabora hadi Isaka kilometa 162.5 na Isaka hadi Mwanza kilometa 311.25,” anafafanua Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa na kwamba awamu ya kwanza ya mradi huo wa reli kutoka Dar es Salaam hadi Makutupora unagharimu Sh trilioni 7.1.Akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo Aprili mwaka huu, Rais Magufuli alisema ili nchi yoyote iweze kujitegemea, ina wajibu wa kumiliki vitu muhimu kama reli, bandari, nishati, barabara, mawasiliano na vingine. Aliongeza kuwa, ujenzi wa reli ya kisasa utaongeza tija na ufanisi katika usafiri wa reli nchini kwani utarahisisha usafirishaji wa mizigo na abiria.Mathalani, safari kati ya Dar es Salaam na Mwanza inayotumia saa 36 kwa usafiri wa reli ya kawaida, sasa itapungua mara nne na kufikia saa 7 hadi 9 tu. Dar es Salaam na Morogoro safari yake itakuwa chini ya saa 1:30 wakati kwenda Dodoma hazitazidi saa 3. Kwa upande wa biashara, inatarajiwa kuimarisha biashara kati ya Tanzania na nchi jirani za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Rwanda, Uganda, Zambia na kadhalika ambazo hazina bahari, hivyo kutegemea kusafirisha mizigo kupitia bandari ya Dar es Salaam.Treni za mizigo zinatarajiwa kubeba tani milioni 17 kwa mwaka. Hii, si tu itapunguza uharibifu wa barabara kutokana na malori ya mizigo, lakini itaongeza pia kasi ya biashara nchini na nchi za jirani pia. Reli ya kisasa ya Tanzania itakuwa na kasi ya kilometa 160 kwa saa, hivyo kuifanya kuwa ya aina yake kwa reli za masafa marefu barani Afrika.Ni ya mizigo na abiria na ina urefu wa kilomita zaidi ya 722 pamoja na njia za kupishania kutoka Dar es Salaam –Morogoro mpaka Dodoma ukitoa njia za kupishania ni zaidi ya kilomita 500 kutoka Dar es Salaam – Dodoma huku ikiwa ni ya mizigo na abiria”. Katika nchi tisa zenye miradi ya SGR barani Afrika, Afrika Kusini, Morocco na Tunisia wamejenga reli ambazo ni fupi zenye urefu wa kilomita 80 mpaka 100 zina kasi kubwa ambayo ni kilomita 200 kwa saa zikiwa treni maalumu kwa abiria tu.
3
Leo Jumamosi ya Tarehe 7 Desembe 2019 kuna michezo mingi kwenye ligi kuu ya Uingereza na michezo hii inaweza kukupa pesa nyingi kama utaitumia vizuri kwenye kubet kwenye mkeka wako Karibu Mdau wa Bongoleo na tunakwenda kutazama namna ya kupata pesa kutokana na ratiba nzima ya soka la uingereza leo Everton Vs Chelsea Usiku wa kuamkia jana Everton walimtikua kocha wao Marco Silva kutokana na kiwango kibovu cha timu na sasa timu hiyo ipo chini ya kocha msaidizi si mbaya kama wachezaji watataka kuonyesha kuwa wanauwezo mkubwa na alikuwa anawaangusha ni kocha tu hivyo wachezaji Everton wataitumia mechi  kama fainali Kwa Upande wa Chelsea mambo yao ni mazuri wamepata ushindi kwenye mchezo wao ukiopita baada ya kucheza michezo motano bila ushindi morali na hali imesharejea kwenye Timu Katika michezo minne ya mwisho kukutanisha timu hizi Everton imeshinda mara moja Chelsea mara moja na sare mara mbili TIP: Ukitaka kubet Mechi hii Weka Both Team To Score (GG) @1.77 Spurs Vs Burnley Unajua Tangu Jose Mourinho achagukiwe kuiongoza Spurs hawajapata clean sheet hata moja na wamefungwa jumla ya magoli nane ndani ya mechi nne tu alizoziongoza Jose Mourinho Burnley wao hali sio mbaya sana lakini katika michezo yao yote wa ugenini wameshinda mchezo mmoja tu TIP : Kama UnaBet mechi Hii Mpes Spurs Ushindi @1.43 Manchester City Vs Manchester United Kama kuna mchezo una magoli wikiendi hii basi mchezo huu kwakua Manchester City ambao wapo nyumbani kwenye michezo yao minne ya mwisho ya nyumbani wameruhisu magoli manne katika mechi tatu na hwajaruhusu kufungwa kwenye mechi moja tu United wao chini Soskjaer wapo vizuri kwenye mechi dhidi ya timu kubwa maana wameshinda mechi tatu kati ya nne ambazo wamecheza na tilu kubwa na hawajapoteza TIP: Kama Unataka Kubet Mechi Hii Weka Both Team To Score (GG) @ 1.86
4
Dk. Fredirick L Mashili, MD, PhD. UNAPOTAKA kufanikisha kuwa na afya njema, mazoezi na lishe bora ni kama baba na mama. Vitu hivi viwili hutegemeana katika kuleta matokeo chanya. Hauwezi kufikia malengo ya kuwa na afya bora bila kuzingatia mazoezi na lishe bora kwa wakati mmoja. Maana yake ni kwamba, hata kama utafanya mazoezi mara kwa mara, lakini lishe yako ikawa mbovu, usitegemee kupata mafanikio makubwa ya malengo yako. Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kufanya mazoezi, lakini wengi wao bado wakilalamika kutokufikia malengo waliyojipangia. Leo tutajadili aina za ulaji na vyakula vinavyoweza kuharibu kabisa juhudi zako za mazoezi na kukufanya usifikie malengo uliyojiwekea hata kama unatimiza viwango vya mazoezi vinavyoshauriwa.   Kula chakula kingi mara baada ya mazoezi Kwa kawaida unapofanya mazoezi mwili hutumia nguvu nyingi. Hii ni mojawapo ya sababu zinazokufanya uhisi njaa na hamu ya kula mara baada ya kufanya mazoezi. Jijengee tabia ya kula mlo mdogo badala ya kula chakula kingi kwa sababu hurudisha mwilini nishati-lishe (calories) ulizozitumia wakati wa mazoezi, hivyo kuondoa faida ulizokuwa umezipata kwa kufanya mazoezi.   Kula chakula kisichofaa baada ya mazoezi Nguvu au nishati-lishe inayokuwa imetumiwa wakati wa mazoezi hukufanya uwe na hamu ya vyakula vyenye sukari, mafuta na wanga. Hii inatokana na mabadiliko ya vichocheo (hormones) yanayoendana na utumiaji wa nishati-lishe mwilini yanayotokea wakati wa mazoezi. Hii ndiyo sababu ya watu wengi kuwa na hamu na vyakula vya aina hii. Lakini ikumbukwe kwamba kula vyakula vyenye sukari na mafuta mengi mara tu baada ya mazoezi si jambo zuri. Epuka vitu kama soda, juice zenye sukari nyingi na baadala yake kula mlo wenye sukari ya asili kiasi, kama vile juisi ya matunda isiyoongezwa sukari. Pia kula mlo wenye kiasi kikubwa cha protini ili kuusaidia mwili kurudi katika hali yake (recovery)   Kula chakula kingi zaidi ya kiasi cha mazoezi unayofanya Watu wengi hudhani kwamba, kwa kuwa wanafanya mazoezi hawana haja ya kujali kiasi na aina ya chakula wanachokula. Ikumbukwe kwamba kinachotakiwa ni uwiano kati ya nishati-lishe inayoingia na ile inayotoka mwilini. Nishati-lishe huingia mwilini kwa njia ya chakula, na hutumika au kutoka mwilini kwa kufanya mazoezi. Kutokana na malengo mbalimbali ni muhimu kufahamu jinsi ya kufikia uwiano utakaokufanya ufaidike. Kwa mfano; endapo lengo lako ni kupungua uzito, ni sharti utumie nishati-lishe nyingi zaidi ya zile unazoingiza mwilini. Maana yake ni kwamba, kiasi na kiwango cha mazoezi kizidi kiasi cha chakula unachokula. Ukikosea uwiano huu huwezi kufaidika na mazoezi.   Kutumia kiasi kidogo cha protini na wanga kwa wingi Mafuta hujengeka na kuongezeka mwilini kutokana na kiasi kikubwa cha nishati-lishe kinachoingia mwilini kama chakula. Vyakula vya wanga na vile vya mafuta hutoa nishati-lishe nyingi zaidi ya vyakula vya protini. Ifahamike pia kwamba uyeyushaji wa vyakula vya protini hutumia nishati-lishe nyingi hivyo kusaidia kutumia nishati-lishe ya ziada mwilini. Kwa maana hiyo, pamoja na kufanya mazoezi vyakula vyenye protini nyingi na wanga kidogo husaidia kuzuia ongezeko la mafuta mwilini.   Kunywa pombe kupita kiasi Pombe ina nishati-lishe nyingi. Kwa maana hiyo unywaji pombe kupita kiwango kilichoshauriwa huchangia katika kuongeza mafuta mwilini. Hata kama unafanya mazoezi kwa kiwango kikubwa, kunywa pombe kupindukia kutarudisha juhudi zako nyuma   Kula chakula kingi chenye wanga wakati wa usiku Wengi wetu hupumzika wakati wa usiku. Kwa maana hiyo hatuhitaji nguvu nyingi mwilini. Kula kiasi kikubwa cha wanga (vyakula vyenye kutoa nishati-lishe nyingi) hutupa nguvu ya ziada, ambayo hatuitumii. Nguvu hii ya ziada hutunzwa mwilini kama mafuta. Kwa maana hiyo, hata kama utakuwa ulichoma mafuta ya kutosha wakati wa mazoezi, kula chakula kingi cha aina ya wanga wakati wa usiku hupoteza juhudi zako za mazoezi.
0
WAKALA wa Ndege za Serikali (TGFA) umesema kuwa fedha zote zilizolipwa kwa ajili ya kuipeleka ndege aina ya Fokker 50 kupakwa rangi nje ya nchi, zimesharejeshwa.Hayo yalibainishwa na Mtendaji Mkuu wa TGFA, Dk Benjamin Ndimila alipozungumza na gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana. Dk Ndimila alisema asilimia 60 ya fedha zilizotakiwa kutumika kwa ajili ya kupaka rangi ndege hiyo ambazo zilishatolewa zimerejeshwa zote.Wakati akimuapisha Valentino Mlowola kuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba pamoja na kupokea taarifa ya mwaka ya utendaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Machi 28, mwaka huu, Rais John Magufuli alifichua mpango wa kutaka kutumia mamilioni ya fedha kupaka rangi ndege hiyo nje ya nchi.Katika maelezo yake, Rais Magufuli alisema watu waliopangwa kusindikiza ndege hiyo walikuwa tayari wameshalipwa dola 28,000 sawa na Sh milioni 60. Alisema gharama ya kazi hiyo ilikuwa Sh milioni 200 na ilipangwa ifanyike katika kipindi cha kati ya siku 15 hadi mwezi mmoja. Mpango huo ambao Rais Magufuli alisema alikuwa akifuatilia hatua kwa hatua, haukufanikiwa kutokana na yeye kuingilia kati na kuwataka wahusika waifanye kazi hiyo hapa hapa nchini.
3
Kauli hiyo aliitoa kwenye mkutano wa hadhara juzi wakati alipokuwa akijitambulisha kwa wananchi katika ziara yake ya kwanza aliyoianza wilayani hapa.Alisema ili wilaya ya Igunga iweze kusonga mbele kimaendeleo ni vema milango ikafunguliwa wazi kwa kampuni mbalimbali ambazo zinaweza kuja kuwekeza hapa kwa kuwa wilaya ya Igunga ni miongoni mwa wilaya zenye madini ya kutosha.Alibainisha kuwa endapo kampuni hizo zitapatikana, wananchi wanaweza kupata ajira kwa kuwa nao watapatiwa fursa ya kutengewa maeneo ya wachimbaji wadogo.Aidha amewataka wananchi wa Igunga kulima mazao ya mtama, mihogo pamoja kunde kutokana na ukame ambao ameukuta katika wilaya ya Igunga kwani endapo mazao hayo yatalimwa kwa wingi yanaweza kuondoa upungufu wa chakula katika wilaya.Wakati huo huo, mkuu huyo wa wilaya ametenga siku maalumu ya usafi katika mji wa Igunga ambayo itakuwa ikifanyika kila Alhamisi ambapo wananchi wote watatakiwa kufanya usafi katika maeneo yao ya biashara na makazi.Zipporah amewaagiza watendaji wa vijiji na kata kuhakikisha wanasimamia ujenzi wa vyumba vya maabara ili viweze kukamilika kwa muda uliopangwa.Naye Mkurugenzi wa mamlaka ya mji mdogo wa Igunga, Pascrates Kweyamba alisema endapo wawekezaji watafika mji wa Igunga itawawezesha kupata mapato kwa wingi kutokana na vyanzo vya madini na vinginevyo.
5
SAKATA la askari polisi wanane wanaodaiwa kujihusisha na kashfa ya utoroshaji dhahabu jijini Mwanza, limetua rasmi kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Boaz.Askari hao ambao Januari 4, mwaka huu, waliwakamata watu waliotaka kutorosha kilo 323.6 za dhahabu yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 30 na fedha taslimu Sh milioni 305, walitaka wapewe Sh bilioni 1 kutoka kwa watuhumiwa hao. Baada ya mpango wao huo kukwama kutokana na mamlaka za nchi kuingilia kati na watuhumiwa kutiwa mbaroni na askari wenzao, kinachoendelea kwa sasa ni uchunguzi wa suala hilo ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani.DCI Boaz, katika mahojiano maalumu na gazeti hili jana, alisema ofisi yake itakamilisha upelelezi wa jambo hilo hivi karibuni. Alisema kuwa upelelezi unaoendelea, utawasaidia kujua ni makosa ya aina gani watuhumiwa hao wanane, wanakabiliwa nayo ili mashitaka dhidi yao yaweze kufunguliwa. Alisema kwa kuwa watuhumiwa hao ni askari, watapelekwa kwanza kwenye Mahakama ya Kijeshi kwa ajili ya mashitaka ya kinidhamu na kama kutakuwa na jinai yoyote dhidi yao, ndipo watakapopelekwa kwenye Mahakama za Kiraia.Wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam juzi, akiwemo Waziri wa Madini, Doto Biteko, makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu, katibu tawala mmoja na makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Rais John Magufuli aliwaeleza Watanzania mpango mzima ulivyokuwa. Kwa mujibu wa Rais Magufuli, askari hao baada ya kuwakamata watuhumiwa, waliwafikisha Kituo Kikuu cha Polisi Mwanza, lakini hawakushushwa kwenye gari, badala yake walichokifanya ni kuwataka watuhumiwa wawepe Sh bilioni 1.Baada ya majadiliano yao, watuhumiwa katika mkupuo wa kwanza, waliwapatia askari hao Sh milioni 300, mkupuo wa pili wakawapa Sh milioni 400 na kuahidi kumaliza mkupuo wa tatu wa Sh milioni 300 watakapofika wilayani Sengerema. Wakiwa njiani kuelekea Sengerema, ndipo walipokutana na kizuizi cha polisi njiani na watuhumiwa wote wakiwemo askari hao wanane wakatiwa mbaroni. Kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na jeshi hilo, Rais Magufuli alimpongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro kwa kazi nzuri iliyofanyika.Ili kufanikisha kazi hiyo ya kufuatilia utoroshaji wa dhahabu na madini mengine nchini, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamanda Ahmed Msangi, alisema kuwa msingi wao mkubwa wa kufanikisha kazi hiyo ni wananchi. Alisema Jeshi la Polisi litafanya kazi kwa karibu na wananchi, ikiwemo kuwapatia elimu ili wananchi hao waweze kushirikiana na jeshi hilo, kwa kutoa taarifa kuhusu utoroshaji huo.
3
Wataalamu hao wakiongozwa na Paolo Mauro, walisema katika taarifa yao jana kwa vyombo vya habari, kuwa hata ukuaji wa uchumi nchini bado ni imara.“Kutokana na mwendelezo mzuri wa sera ya fedha na wa bei za vyakula katika kanda, mfumuko wa bei unatarajiwa kushuka zaidi katikati ya mwaka huu hadi kufikia lengo la muda wa kati la asilimia 5,” ilisema taarifa hiyo.Iliongeza kuwa nakisi ya urari wa mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi iliongezeka zaidi mwaka jana, kutokana na kupungua kwa bei za mauzo ya dhahabu na mazao asilia katika soko la dunia.Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/13, iliongeza taarifa, kulijitokeza matumizi makubwa ya Serikali kuliko ilivyotarajiwa na kusababisha kiwango halisi cha ukopaji wake, kutoka taasisi za ndani kuzidi lengo lililokubaliwa chini ya mpango wa Serikali na IMF kwa asilimia 1.2 ya Pato la Taifa.“Katika mwaka huu wa fedha (2013/14), makusanyo ya mapato yanaendelea kuwa chini ya makadirio yaliyoingizwa katika bajeti iliyopitishwa na Bunge.“Ili kufikia nakisi ya bajeti ya karibu na asilimia 5 ya Pato la Taifa, Serikali imechukua hadhari katika kupeleka fedha kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti,” ilisema taarifa.Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wakati wa mapitio ya utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha nusu mwaka, inatarajiwa mgawo wa matumizi kupunguzwa ili yaendane na makusanyo ya mapato. Wakati huo huo, malimbikizo ya madeni yameongezeka kwa kiasi kikubwa, hasa kwa miradi ya barabara.Ilishauriwa kuwa ili kutunza heshima ya mchakato wa bajeti na sera ya fedha, hatua zaidi za kisera zinahitajika ili kuepuka malimbikizo mapya na kulipa yaliyopo baada ya ukaguzi."Kuendeleza utulivu wa uchumi ni muhimu kwa ajili ya uchumi kuendelea kukua kwa haraka katika kipindi cha muda wa kati … changamoto kubwa ni kuendelea kuiwezesha bajeti kukidhi uwekezaji katika miundombinu na matumizi kwa ajili ya vipaumbele vya jamii, na wakati huo huo kuendelea kupunguza nakisi ya bajeti ili kulifanya deni la Taifa kuendelea kuwa himilivu,” ilisema IMF.Mageuzi yanayoandaliwa katika sera za kodi za Serikali ikiwa ni pamoja na mapitio ya sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) yana uwezo wa kuongeza ufanisi na kukusanya mapato zaidi na kuleta usawa katika kugawana mzigo wa kodi, ilisema.Hata hivyo, uzoefu katika mwaka huu wa fedha wa makusanyo ya mapato yasiyotosheleza matumizi, vinapaswa vitumike kuona umuhimu wa kuwa na makadirio halisi ya mapato katika mzunguko ujao wa bajeti."Makubaliano yalifikiwa katika ngazi ya wataalamu juu ya hatua za kisera ambazo zitachangia kuhitimisha mapitio ya mwisho chini ya mpango mpya wa Ushauri wa Sera za Uchumi (SCF). Uhakiki wa mwisho unategemea idhini ya Baraza la Mawaziri na Bodi Tendaji ya IMF.“Makubaliano ya jumla yalifikiwa kwenye muhtasari wa mpango ambao hatimaye unaweza kuwa mpya wa PSI wakati ikisubiri kukamilika kwa majadiliano ya kina,” ilisema.Taarifa ilieleza kuwa mkutano ujao wa Bodi Tendaji ya IMF kuhusu Tanzania umepangwa kufanyika mwishoni mwa Aprili.“Timu ya wataalamu wa IMF inatoa shukrani kwa majadiliano ya uwazi na yenye tija kwenye masuala ya kisera na kwa ukarimu wa dhati wa Serikali,” ilihitimisha taarifa hiyo.Ujumbe huo wa IMF ulikutana na Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu na maofisa waandamizi wa Serikali.
5
SERIKALI imeuagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuendelea kuwaruhusu wenye viwanda vya mbao watumie mashine za zamani za kuchakata mbao, huku wakiendelea kujipanga kununua mashine za kisasa kulingana na mabadiliko ya teknolojia.Hatua hiyo inakuja baada ya zuio la wamiliki wa viwanda hivyo kutumia mashine za zamani za kuchakata magogo ambazo zimekuwa zikizalisha taka nyingi, hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa mbao.Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu wakati alipozungumza na wadau wa misitu wa wenye viwanda vya mbao katika shamba la miti la Longuza wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.Mwenyekiti wa Wamiliki wa Viwanda vya mbao kwa mikoa ya Kaskazini, Ibrahimu Shoo alilalamikia zuio hilo huku akimuomba Naibu Waziri huyo kuwa awape muda wa kutosha kwa ajili ya kujipanga kununua mashine za kisasa.Kutokana na malalamiko hayo, Kanyasu aliielekeza TFS iendelee kutoa leseni na mgao wa vitalu vya miti kwa wamiliki wa viwanda wenye mashine za zamani, ili kuweza kutoa fursa kwao kuweza kujipanga kununua mashine ambazo zinazalisha taka chache wakati wa uchakataji wa mbao.Hata hivyo, waziri huyo aliwaeleza wadau hao kuwa maamuzi ya mashine za kisasa za kupunguza hasara ya upotevu mkubwa wa mbao bado yapo palepale.Aidha, alisema maamuzi ya kuwataka wamiliki wa viwanda vya mbao kutumia mashine hizo mpya linakwenda sambamba na zuio lililokuwa limetolewa siku za nyuma la kuzuia kutumia misumeno ya Dingdong ambayo nayo ilikuwa ikisababisha upotevu mkubwa wa mbao.Pia, aliagiza TFS itoe mikataba ya miaka miwili kwa wamiliki wa viwanda vya mbao hali itakayowasaidia kutoa uhakika kwao, hivyo kuweza kukopesheka katika benki nchini.Alifafanua kuwa benki zilizo nyingi zimekuwa zikitoa mkopo wa muda wa miezi 12 hali itakayowasaidia wafanyabiashara hao kuwa na uwezo wa kurudisha pesa walizokuwa wamezikopa endapo wataweza kupewa mikataba ya muda wa miaka miwili.Katika hatua nyingine, Kanyasu aliwataka wadau wa misitu nchini hasa wenye viwanda vya mbao wafungue mashamba makubwa ya miti ili baadaye waanze kuvuna miti katika mashamba yao hali itakayosaidia kupunguza utegemezi kutoka kwenye mashamba ya miti ya serikali.Alisema nchi kama Finland uchumi wao unategemea kwa kiasi kikubwa misitu na wamiliki wakubwa wa mashamba ya miti ni wadau wa misitu wa nchi hiyo.
3
ZIKIWA zimebaki siku mbili michuano ya Kombe la Chalenji (Cecafa) kwa wanawake kuanza kutimua vumbi nchini, mambo yamezidi kuiva kwa timu shiriki kutoka nje kuanza kuwasili tayari kwa michuano hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.Akizungumza jana jijini Dare es Salaam, Katibu wa Chama cha Soka la Wanawake nchini, Somoe Ng’itu, alisema michuano hiyo inashirikisha timu nane zilizopangwa katika makundi mawili ya A na B na kwamba maandalizi ya mapokezi kwa timu shiriki yanaenda vizuri.Alisema hadi sasa ukiwatoa wenyeji Kilimanjaro Queens , timu nne ambazo ni Burundi, Kenya, Djibout na Ethiopia zimeshawasili nchini tangu jana na leo zinatarajia kutua timu za Uganda, Sudan Kusini na Zanzibar.“Maandalizi yanaenda vizuri kama tulivyopanga na hadi sasa tumeshapokea timu nne, ambazo ni Burundi, Kenya, Ethiopia na Djibout na nyingine tatu tunatarajia kuzipokea kesho (leo), ambazo ni Uganda, Sudan Kusini na Zanzibar tayari kwa michuano itakayoanza Jumamosi, “ alisema.Ng’itu alisema maandalizi ya michuano hiyo yamekamilika sambamba na viwanja vya kufanyia mazoezi kwa timu hizo, ambapo wameanda viwanja vitatu vya Azam Complex Temeke, Karume na JMK Park Kidongo Chekundu, vyote vya Ilala .Timu hizo zimepangwa kwenye makundi mawili, ambapo Kundi A lina timu za Kilimanjaro Queens ambao ni wenyeji na mabingwa wa tetezi mara mbili mfululizo na timu za Zanzibar, Burundi na Sudan Kusini, wakati Kundi B linaundwa na timu za Ethiopia, Kenya, Uganda na Djibout.Michuano hiyo inayodhaminiwa na Baraza la Vyama vya Soka Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho hadi Novemba 27.
4
TAASISI za tafiti wa afya imetakiwa kubuni na kufanya kazi za tafiti za kina zitakazoibuwa na kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wananchi ikiwemo maradhi yasiyoambukiza ambayo ni tishio kwa afya za wananchi.Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi ametoa changamoto hiyo wakati akizindua kituo cha utafiti wa tiba za dawa na maradhi yanayowakabili wananchi huko Binguni wilaya ya kusini Unguja katika shamra shamra za Mapinduzi ya Zanzibar.Alisema kwa mfano hivi sasa yamezuka maradhi mbalimbali yasiyoambukiza ambayo ni tishio kwa afya za wananchi na kusababisha vifo.Alisema kuwa tafiti zaidi na za kina zinahitajika katika kukabiliana na maradhi hayo pamoja na tiba asilia inayotokana na mimea mbalimbali.“Kituo hiki ni muhimu na tegemeo kubwa katika kufanya kazi za utafiti wa maradhi mbali mbali ambayo ni tishio kwa Afya za wananchi yanayosababisha vifo vya wananchi wengi na wengine kupata ulemavu wa kudumu,” alisema.Kwa mfano alisema utafiti zaidi unahitajika kuweza kupambana na ugonjwa wa Kisukari kwa kujuwa chanzo chake na tiba ya aina mbali mbali ikiwemo ya mimea ya miti shamba.“Zipo taarifa kwamba maradhi yasiyoambukiza yanaongoza kwa vifo vingi hivi sasa ikiwemo ugonjwa wa Kisukari ambao pia husababisha ulemavu wa kudumu,” alisema.Mapema Katibu Mkuu Wizara ya Afya Asha Ali Abdalla alisema serikali imeweka kipaumbele masuala ya utafiti katika mambo mbalimbali ili kuyapatia ufumbuzi wake.Kwa mfano alikiri hivi sasa kuwepo kwa maradhi mengi yasiyoambukiza ambayo yamekuwa tishio kwa afya za wananchi na kusababisha ulemavu wa kudumu.Alisema kitengo hicho miongoni mwa kazi zake za kufanya ni kushughulikia mambo ya utafiti wa maradhi ili kujuwa chanzo na njia za kupambana nayo.“Katika mambo ambayo yamepewa kipaumbele ni utafiti ambao utalenga katika kuzipatia ufumbuzi kero mbali mbali zinazowakabili wananchi katika masuala ya afya,” alisema.Ujenzi wa kituo cha utafiti wa afya umegharimu jumla ya Sh milioni 210 ambapo miongoni mwa majukumu yake ni kufanya utafiti na kuchunguza maradhi mbalimbali yanayowakabili wananchi.
3
ABDULAH MKEYENGE YANGA, Azam Fc zimetoa orodha ya wachezaji waliowaacha. Katika orodha hizo wachezaji vijana ni wengi. Ni wengi mno. Kiufupi tu. Yanga imemuacha Deus David Kaseke, Azam Fc imemuacha Ramadhan Singano. Nasikia mashabiki zake wamembatiza jina la Messi. Sijali sana. Wengi wameachwa wakiwa hawajafikisha miaka 26 kwa mujibu wa taarifa zao zilizoko Google. Kuna tatizo sehemu. Haiwezekani. Wakati haya yakiwatokea kina Kaseke, mikataba ya kina Juma Kaseja ( KMC), Mrisho Ngassa, Kelvin Yondani (Yanga), Agrey Morris (Azam Fc), Shaban Nditi (Mtibwa Sugar FC) iko salama. Kuna kitu cha kujifunza. Kuna darasa la bure hapa. Ina maana vijana wameshindwa kuwastahafisha wakongwe badala yake wakongwe wamegoma kuzeeka na wanalinda nafasi zao, mpaka vijana wanaachwa? Ni swali letu vijana tujiulize kwa pamoja. Wapi tunapokwama mpaka yanatukuta? Kuna muda huwa najisemea ni wakati wa Yondani na Morris kupisha damu mpya katika ukuta wa Stars, lakini kila nikigeuka kulia na kushoto kutazama vijana wa kuwafanya Yondani na Morris wasicheze siwaoni. Nimetazama hili mara nyingi. Mwisho wa siku macho yangu yanarudi pale pale kwa kina Yondani na Morris. Lakini ukweli mchungu ni kwamba vijana wa lika langu ni wavivu wa mazoezi magumu. Hawapendi kuambiwa haya tunayoyaandika. Wanapenda kusifiwa tu na mazoezi yao ni mepesi ambayo mwanangu hayamshindi. Wamezoea kula kiwepesi. Jioni moja katika korido za Uwanja Taifa nilimsikia Yondani akisema anatamani kuacha kucheza Stars lakini hakuna mchezaji wa kumfanya astahafu. Niliibeza kauli ile, nikahisi Yondani anajisifu, lakini baadae nilivyoifikiria nje ya 18, nikajiona mjinga. Yondani alizungumza ukweli. Huu ni ukweli ambao vijana wengi hawapendi kuusikia ukipenya kwenye ngoma za masikio yao. Tumebaki kusema fulani mchawi. Tunaamini uchawi katika jambo la Kisayansi. Mpira ni Sayansi, uchawi unaingiaje? Kama mpira ni uchawi, basi wachawi wa kwanza ni vijana wenyewe. Uchawi wenyewe unaanzia hapa. Vijana hawapati muda maalum wa kupumzika, hawali vyakula vya kujenga miili, hawapendi mazoezi magumu. Huu ni uchawi mbaya tusioujua. Ni kocha gani akupange wewe kijana uliyechelewa kulala kwa sababu ya disko amuache nje mkongwe aliyelala mapema. Akala vizuri na anapenda mazoezi magumu? Hakuna kocha huyo. Kama vijana wanataka kuwatoa wakongwe katika nafasi zao ni lazima mienendo yao ibadilike ili mwisho wa msimu tuone idadi kubwa ya majina ya wakongwe yakikatwa, lakini kama wataendelea kuwa hivi nawaona wakongwe wakizidi kuwa wachezaji muhimu katika timu. Pale unapomuona Kaseja na kujiridhisha kuwa amefikia mwisho, mwenzako anajiona yuko fiti na yuko fiti kweli. Mazoezi yamemfanya Kaseja kila siku aonekane mpya mbele ya mboni za watu. Mungu akinipa pumzi msimu ujao nitaenda kumuona George Kavila akicheza ligi kwa mwaka wa 22 mfululizo. Vijana wengi wamemkuta katika soka la ushindani, cha ajabu wamemuacha. Kavila wa miaka 10 iliyopita ndiyo Kavila wa leo. Hana makuu yuko vile vile. Anajitambua. Anajitunza. Sitaki kutaka maji mengi ya watu. Jikumbushe kuhusu Said Bahanuzi. Nani anajua aliko? Binafsi sijui kama kaacha soka au anafanya kazi gani. Huyu Mbwana Samatta tunayemtazama kama kioo chetu hajafika Genk kwa bahati mbaya kama tunavyodhani. Aliamua kuacha kazi akafanya kazi, leo hii Wazungu wanaliimba jina lake na kumtukuza. Ni kama ‘Mungu’ wao wa mabao. Muda huu ambao Singano anapishana na Morris katika chumba cha kusaini mikataba cha Azam, mkononi akiwa na barua yake ya kuachwa, huku Kaseke akipishana na Boban katika chumba hiko naye akiwa na barua hiyo, kuna kiujumbe fulani cha kuondoka nacho kwa hawa vijana wenzetu. Uncle Jerson Tegete nakusalimu uncle. Swalamaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!
4