text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
Na Leah Mushi, Afrika Kusini Mwanaharakati wa Masuala ya Wanawake na Watoto wa Afrika, Mama Graca Machel amesema ni wakati sasa kwa taifa la Afrika Kusini kuwaita mashujaa wa taifa, kuwashukuru na kuwaenzi wakiwa hai kwa kuwa hakuna ajuaye kama wanasikia na kuona vile wanavyosifiwa wakati wa misiba yao. Aidha, amekemea tabia ya jamii kuwananga na kuwasema watoto wa wapigania uhuru kwa kuwa wengi wao wamekosa miongozo na malezi bora ya wazazi kwani wazazi hao walikuwa na ujasiri wa kuacha familia zao na kupigania taifa hivyo si sawa kuwasema na kuwanyooshea vidole badala yake waoneshe upendo zaidi kwao katika kile kilichofanywa na wazazi wao. Akizungumza mbele ya umati wa watu kutoka maeneo mbalimbali duniani waliofika kutoa salamu za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Winnie Mandela ambaye amekuwa akimuita dada mkubwa, aliyefariki dunia Aprili 2, mwaka huu nchini Afrika Kusini. Pamoja na mambo mengine, Mama Graca ambaye pia ni mjane wa Rais wa zamani wa afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela, amezungumzia kuhusu rambirambi na ahadi zinazotolewa misibani ambapo amewataka wananchi na wanasiasa kuacha maneno ya hadaa kwani mengi yanayoahidiwa hayatekelezwi. “Kwa sasa ukiangalia Afrika Kusini mambo yamekuwa mabaya zaidi kuliko Mandela alipokuwa hai, na hii inaonesha kiasi gani watu hawaishi ahadi zao walizoahidi na ndiyo jambo hata leo watu wengi wameahidi kuendeleza harakati za Winnie Mandela lakini nani anajua kama zitatekelezwa?” amehoji mama Grace. Hata hivyo, ameitaka jamii kwa ujumla kuamka na kusaidia kuinua jamii kwa kuwa zaidi ya asilimia 50 ya wananchi ni masikini na hakuna juhudi za mmoja mmoja za kulikomboa taifa katika tatizo hilo badala yake kila mtu anaitupia lawama serikali. “Ebu jiulize, ni namna gani shujaa wa taifa angejisikia pale ambapo amekaa mbele ya watu wa rika tofauti jinsia tofauti wenye mirengo tofauti ya kisiasa wote wakimsifia na kumshukuru kwa werevu wake wa kulipigania taifa?” amesema. Katika hotuba yake hiyo aliyoitoa kwa zaidi ya nusu saa, Mama Graca ameahidi kutomzungumzia  Winnie Mandela kwa kuwa kila mtu amekuwa akifanya hivyo na badala yake kuitaka jamii kubadilika. Mama Graca Machel ambaye alikuwa mke wa Nelson Mandela tangu mwaka 1998 mpaka mauti yalipomkuta mwaka 2013 alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Winnie Mandela na wamekuwa wakishirikiana katika masuala mbalimbali ya kutetea haki za raia nchini Afrika Kusini na Afrika kwa ujumla.
2
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amekagua mradi wa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mbinga kwenda Mbamba Bay, yenye urefu wa kilomita 69 itakayogharimu sh. bilioni 129.3.Majaliwa alikagua barabara hiyo jana wakati akielekea wilayani Mbinga kwenye ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Ruvuma. Waziri Mkuu alisema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo wa barabara inayojengwa na kampuni ya Chico ya nchini China, ambapo aliagiza uongozi wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kusimamia vizuri mradi huo. “Kazi hii inafanywa kwa uhodari mkubwa, naipongeza kampuni ya Chico kwa hatua waliyoifikia na ninaamini kwamba barabara hii inayotarajiwa kukamilika Januari 2021 itakamilika mapema zaidi” alisema.Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme alisema kukamilika kwa barabara hiyo, kutachochea ukuaji wa uchumi kwa wananchi na mkoa kwa ujumla, kwani itarahisisha usafiri wa watu na mizigo.Alisema pia barabara hiyo itakuza sekta ya utalii na uvuvi katika mkoa wa Ruvuma kwa sababu itawezesha watalii na wafanyabiashara, kufika kwa urahisi katika wilaya ya Nyasa, ambayo ni kiungo cha biashara kati ya nchi jirani na mikoa inayopitiwa na ziwa Nyasa. Mndeme alimshukuru Rais John Magufuli kwa kuwapelekea fedha za ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ya hospitali, vituo vya afya, shule, nishati na maji.
3
RIO DE JANEIRO, BRAZIL WENYEJI wa michuano ya Olimpiki, Brazil, tayari wameyaaga mashindano hayo kwa upande wa timu ya taifa ya mpira wa miguu. Timu hiyo ya wanawake ilikuwa na ndoto ya kufanya vizuri kwenye viwanja vya nyumbani na kutwaa medali za dhahabu, lakini ndoto hizo zimefutwa baada ya kupokea kichapo cha mabao 4-3 ya mikwaju ya penalti dhidi ya wapinzani wao kutoka nchini Sweden. Mchezo huo wa nusu fainali uliopigwa usiku wa kuamkia jana, ulimalizika dakika 90, huku timu hizo zikiwa hazijafungana, hivyo waliongeza dakika 30 lakini hakupatikana mbabe ndipo wakaenda kwenye matuta. Hata hivyo, timu hizo zilipokutana katika hatua ya awali, Brazil ilifanikiwa kushinda mabao 5-1 hatua ya makundi, hivyo Brazil waliamini kuwa watapata nafasi ya kufika fainali, lakini ndoto hizo zimefikia mwisho. Kocha wa timu ya taifa ya Sweden, Pelle Olsson, anaamini ana nafasi ya kuwa bingwa katika michuano hiyo baada ya kufanya vizuri akiwa na timu ya taifa ya United States na kutwaa medali za dhahabu mwaka 2008 na 2012, na sasa anaamini ana nafasi ya kuendeleza ubabe huo huku akiwa na timu hiyo. Timu hiyo inatarajia kukutana na Ujerumani katika mchezo wa fainali, huku Ujerumani ikiingia kwenye hatua hiyo baada ya kuichapa Canada mabao 2-0 kwenye hatua ya nusu fainali, wakati huo Brazil wakitarajia kucheza na Canada kumtafuta mshindi wa tatu ambaye atapata medali ya shaba. Hata hivyo, katika soka la wanawake Brazil haijawahi kupata medali ya dhahabu, hivyo mwaka huu walikuwa na uhakika wa kuipata, wakati huo kwa upande wa Sweden, hii itakuwa ni fainali yao ya kwanza tangu mwaka 1948, ambapo timu ya taifa kwa upande wa wanaume ilifanikiwa kutwaa medali ya dhahabu.
4
TP Mazembe iliyocheza nusu fainali mwaka jana, iliepuka kipigo cha mechi ya kwanza cha bao 1-0 ugenini Tshwane na juzi kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 nyumbani kwake mjini Lubumbashi.Lakini mabao ya Rainford Kalaba, Samata na Roger Assale yalihakikisha kuwa bao la Percy Tau halikuwa na maana kwa wageni hao na hivyo kikosi hicho kusonga mbele.Kwa upande wake, Al Hilal ya Sudan iliitupa nje mabingwa wa Malawi, Big Bullets saa chache baada ya mabingwa hao kupata kifo cha beki wao, Douglas Chirambo.Chirambo aliripotiwa kufariki kwa ugonjwa wa uvimbe kwenye ubongo baada ya kuugua kwa muda mrefu, lakini mechi hiyo ya raundi ya pili iliendelea kama kawaida na kumalizika kwa sare ya bao 1-1, na Wasudan kufuzu kwa jumla ya mabao 5-1.Ushindi wa mabao 4-0 mjini Khartoum yalihakikisha Al Hilal inasonga mbele raundi ya ijayo na walimaliza kazi baada ya Frank Boubacar kusawazisha bao la James Chilapondwa aliyefunga kwa penalti katika dakika ya 74.CS Sfaxien pia iliyofungwa katika nusu fainali msimu uliopita, ilijiweka pazuri baada ya kuishinda Semassi kwa bao 1-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 6-0.Marius Noubissi alifunga bao pekee la mechi hiyo ya marudiano ambayo ilikamilisha ratiba baada ya timu hiyo ya Tunisia kushinda mabao 5-0 mwezi uliopita.Kaloum Star pia imesonga mbele baada ya kuishinda Zesco United ya Zambia kwa penalti 5-4, baada ya timu hizo kumaliza dakika 120 zikiwa sare ya mabao 2-2.Kadi nyekundu ya Kingsley Sokari iliigharimu Enyimba kwani Smouha ya Misri ilifunga mabao mawili katika dakika saba za mwisho kupata ushindi wa mabao 2-0 na kusonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1.Raja Casablanca, Leopard, Esperance Tunis, Sanga Balende na Eulma pia zilisonga mbele juzi.
4
Simba ililazimishwa sare ya mabao 2-2 na Mbao FC kwenye mchezo wa mzunguko wa nne wa ligi hiyo uliopigwa Alhamisi iliyopita Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza matokeo yaliyowashusha hadi nafasi ya nne kwenye msimamo.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Mayanja alisema kuelekea kwenye mchezo huo moja ya mikakati yao ni kuhakikisha wanawatumia washambuliaji wanne, na kucheza kwa kushambulia muda wote wa mchezo jambo ambalo anaamini litawasaidia kupata ushindi.“Unajua kama tutacheza kwa kuwashambulia wataogopa kuja langoni kwetu hiyo itakuwa faida kwetu lakini sababu ya kutumia washambuliaji wanne ni kutaka kufunga mabao mengi iwezekanavyo kama tulivyofanya kwenye mchezo na Ruvu Shooting,”alisema Mayanja.Kocha huyo raia wa Uganda alisema, wamedhamiria kuondoka na pointi tatu katika mchezo huo, na wasingependa kupata sare au kupoteza kwa sasa kwani ushindani umekuwa mkubwa na kila timu imepania kufanya vizuri msimu huu.Mayanja alisema wanawaheshimu Stand kuwa ni timu nzuri na wana rekodi nzuri hasa wanapokuwa kwenye uwanja wao wa nyumbani, lakini watajitahidi kuhakikisha wanacheza kwa nguvu na kupata pointi tatu ambazo anaamini zitapunguza presha waliyonayo kwa sasa.Simba inayofundishwa na Kocha Mkuu Joseph Omog, raia wa Cameroon, inalazimika kushinda mchezo huo, ili kutuliza presha za mashabiki wa timu hiyo ambao wameanza kuutilia mashaka uwezo wake wakidai anapata shida kwenye kusoma mchezo na kufanya mabadiliko hasa baada ya sare ya mabao 2-2 na Mbao.
4
MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeshawalipa wastaafu 10,000 Sh bilioni 880 tangu ulipoanzishwa baada ya serikali kuunganisha mifuko kadhaa ya hifadhi ya jamii.Meneja Kiongozi wa Uhusiano wa mfuko huo, Eunice Chiume alisema hiyo ni hatua kubwa ya mafanikio akiwataka wastaafu hao kuendelea kutoa ushirikiano stahiki kwa maendeleo ya mfuko.Alisema mfuko umeshalipa malimbikizo ya wastaafu waliorithi kutoka mfuko uliokuwa ukiwahudumia wastaafu hao wa PSPF kabla ya kuunganishwa kwa mifuko mingine, malimbikizo ya miaka miwili.Eunice alisema malimbikizo hayo ni Sh bilioni 119 baada ya kurudi kwenye kikokotoo cha zamani na hadi Machi mwaka jana wastaafu waliokuwa wameshahakikiwa walifikia 114,000 waliobaki ni 10,500. Aliongeza kuwa mfuko unawasihi wastaafu hao kuendelea kuhakiki kwenye ofisi za PSSSF zilizopo nchi nzima ili warejeshwe kwenye daftari la wastaafu na hatimaye kulipwa stahiki zao.Eunice alisema mfuko huo umejipanga kuhakiki wastaafu hata wale ambao ni wagonjwa kwa kuwafuata mahala popote walipo. Alisema mfuko unaendelea kungojea barua kutoka waajiri wa watu 227 waliowaajiri kama wafanyakazi wao ambao wengine walistaafishwa kutokana na sababu kadhaa wakiwamo wa vyeti feki waliotimuliwa.“Tunaendelea kungojea ba- rua za uthibitisho kutokea kwa waajiri wao ili tujue nini cha kufanya kwa kuwa wapo ambao wamejikwaza tunashindwa kuwalipa, wakiwamo wa vyeti feki na wengineo,” alisema.
3
UGANDA imeanza kutimiza ndoto ya kutengeneza magari yake yenyewe, badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi na sasa yapo katika majaribio.Hatua hiyo ya kupigiwa mfano, inadhihirisha nia ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ya kutaka kupunguza uagizaji wa magari kutoka nje. Uganda, kupitia kampuni yake umma ya Kiira Motors Corporation (KMC) ambayo kwa kiasi kikubwa inamilikiwa na serikali, imekamilisha kutengeneza moja ya magari yake, aina ya Kiira EVS na tayari limeanza kufanyiwa majaribio katika miji mbalimbali ya Uganda. Gari hilo dogo linalotumia mafuta, linatarajiwa kufanyiwa majaribio kwa umbali wa kilometa 1,600.Mengine, aina ya Kiira EVE linalotumia umeme pekee, na jingine aina ya Kayoola ambalo ni basi linalotumia nishati ya umemejua, tayari yameshatengenezwa na kuingizwa katika hatua mbalimbali za majaribio. Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa KMC, Allan Muhumuza, amethibitisha kuanza kwa majaribio hayo katika Jiji la Kampala na baadaye Masaka, Mbarara, Kabale na Kisoro. Aidha, linatarajiwa kuendeshwa pia hadi Magharibi mwa nchi. “Tumeandika historia. Kote tulikopita, kuanzia Kampala, watu hawaamini kama ni gari lililotengenezwa katika ardhi ya Uganda.Tunatarajia kuendelea na majaribio kwa kilometa 1,600 zaidi,” alisema Muhumuza aliyeongeza kuwa, baada ya majaribio wanajipanga kutengeneza magari mengi zaidi kwa ajili ya soko la Afrika Mashariki na nchi nyingine kupitia kiwanda chao kinachojengwa katika eneo la kilometa 100 katika wa Jinja. Nchi nyingine za EAC kama Tanzania, zina magari yake.Mfano Tanzania ina kiwanda cha magari ya Nyumbu ambacho hutengeneza zaidi magari ya kijeshi. Kenya na Rwanda pia zimo katika ujenzi wa viwanda vya kisasa, vikiwemo vinavyotengeneza na kuuza nje ya nchi magari binafsi, ya kubeba ya watalii, malori ya takataka na pikipiki za aina mbalimbali. Kwa Uganda inayoagiza wastani wa magari 50,000 kwa mwaka, kuunda magari yake yenye alama ya ndege Korongo au Crane anayepatikana pia katika alama zote za taifa, ikiwa ni pamoja na bendera na fedha, ulikuwa mpango wa muda mrefu na sasa umeiva baada ya Rais Yoweri Museveni kuingilia kati na kuagiza kazi za ujenzi wa kiwanda ianze mara moja.Wazo la ujenzi wa kiwanda cha uzalishaji wa magari, lilianza mwaka 2011 baada ya juhudi na maarifa ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Makerere kutengeneza gari linalotumia umeme la Kiira EV na basi linalotumia nishati ya jua la Kayoola EV mwaka 2016. Kutokana na mafanikio hayo ya wanafunzi wa chuo hicho kikubwa barani Afrika, mwaka 2014 serikali ilitenga kipande cha ardhi Mashariki mwa Jinja kwa ajili ya KMC.Mradi huo mkubwa katika historia ya Uganda, unatarajiwa kutengeneza nafasi za ajira za moja kwa moja zaidi ya 2,000 na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 12,000. Kiwanda hicho kitakapokamilika na kuanza uzalishaji wa magari, Uganda itapata soko kubwa katika nchi za Afrika Mashariki kutokana na mahitaji makubwa ya magari. Afrika Mashariki huagiza magari 250,000 kwa mwaka na mahitaji yanatarajiwa kupanda hadi kufikia magari 500,000 kufikia mwaka 2030.Magari ya Tanzania Nchi hii kubwa kuliko zote Afrika Mashariki, ina kiwanda chake kinachotengeneza magari ya nyumbu ambacho ni mali ya Serikali. Aidha, kampuni binafsi, mathalani Hanspaul Automechs Limited (HAL) iliyopo eneo la viwanda Njiro jijini Arusha, inatengeneza magari makubwa ya kubeba watalii maarufu kwa jina la ‘War Bus’.Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Satbir Hanspaul, yanauzwa Kenya, Afrika Kusini na nchi za Ulaya. Kampuni hiyo imebuni na kutengeneza pia magari maalumu ya kubeba taka, yanayofaa kwa mazingira ya Tanzania, ikiwemo hali ya hewa, aina ya barabara na mfumo wa maisha wa wananchi wake.“Lakini aina mpya ya malori ya kubeba takataka si kwa ajili ya kampuni yetu au kiwanda chetu tu, kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa na TBS (Shirika la Viwango Tanzania), wazalishaji wengine wanaweza kuyatengeneza lakini kwa kutumia utambulisho wa ubunifu wa HAL kama kielelezo,” alisema Hanspaul. Alisema, magari ya kubeba takataka na yale ya watalii ni ubunifu wa Tanzania unaozivutia nchi nyingine zikiwemo za Ulaya na magari ya watalii yanakubalika kwenye soko la kimataifa. Kwa mwezi huweza kutengeneza zaidi ya magari 35.“Watu wengi hawataamini kwamba, nchi zenye viwanda vya kutengeneza magari kama Afrika Kusini na zile za Ulaya sasa zinanunua magari kutoka Tanzania, lakini wanafanya hivyo,” alisema. Magari hayo yenye nembo za Toyota, Nissan na Land Rover, yanatengenezwa kwa kutumia mashine za kisasa zikiwemo roboti kama ilivyo kwenye viwanda vya magari katika nchi zilizoendelea. HAL ilianzishwa mwaka 2007 na imelenga kuteka asilimia 25 ya soko la magari na spea zake katika nchi za EAC.Gari la kwanza RwandaGari la kwanza kutengenezwa katika ardhi ya Rwanda liliingia barabarani Juni, mwaka jana. Ni matunda ya kampuni ya Volkswagen (VW) ya Ujerumani ambayo imeamua kutengeneza aina tatu za magari madogo nchini humo, ya Volkswagen Passat, Volkswagen Polo na Volkswagen Teramont.Ofisa Mtendaji Mkuu wa VW Afrika Kusini, Thomas Schafer mwanzoni mwa mwaka huu alisema uwekezaji wa Dola za Marekani milioni 20 ni matunda ya upembuzi yakinifu uliofanywa na kuonekana ni mradi `utakaolipa’ kwa nchi za EAC. Kufikia mwishoni mwa mwezi huu, itakuwa imekamilisha kutengeneza magari 90 na kwamba dhamira katika siku za baadaye ni kutengenea kati ya magari 1,000 na 5,000 kwa mwaka huku ajira zinazotarajiwa kuzalishwa ni kati ya 500 na 1,000.Volvo yaingia KenyaMoja ya kampuni kubwa katika utengenezaji wa magari ya aina mbalimbali, Volvo imeingia nchini Kenya na kuwekeza Sh bilioni 2.5 za nchi hiyo ili kufanikisha ujenzi wa kiwanda kinachotarajiwa kuanza na uzalishaji wa magari 500 kwa mwaka na baadaye kufikia magari 2,000 kwa mwaka.Kiwanda hicho kilichoingia ubia na kampuni ya NECST Motors ya Kenya, kinatarajiwa kuzalisha ajira 300 za moja kwa moja kiwandani hapo, lengo likiwa kushika asilimia 20 ya soko la Afrika Mashariki. Ni kiwanda cha tatu barani Afrika, vingine vikiwa Morocco ambako imeshika asilimia 20 ya soko na Afrika Kusini inakoshika asilimia 18 ya soko la magari.Kwa Kenya, kitakuwa kiwanda cha nne cha magari. Volkswagen kimeanza tena kazi baada ya kusitisha uzalishaji miaka 40 iliyopita. Kampuni za Peugeot, Toyota, wameanza pia uzalishaji, huku Iveco, Ashok Leyland pia wakitangaza nia ya kuanza uzalishaji wake nchini Kenya.
3
Mwandishi wetu-Dar es Salaam Mkazi wa Ifakara, mkoani Morogoro, Gadi Mwajeka (37) ambaye pia shabiki wa timu ya Real Madrid ameshinda kiasi cha Sh 208, 574, 790 baada ya kubashiri kwa usahihi mchezo wa Perfect 12 wa kampuni ya M-Bet. Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi,  Mwajeka  amesema kuwa hakuamini mara baada ya kupigiwa simu kuambiwa kushinda kiasi kikubwa cha fedha. Mwajeka ambaye ni mfanya biashara ya rangi za mkeka Ifakara mjini amesema kuwa ushindi huo ni faraja kubwa sana kwake kwani utamwezesha kuipanua biashara yake na kuanzisha nyingine. “Sikuamini kama nimeshinda kiasi kikubwa cha fedha, nimetumia kiasi cha sh1,000 tu kubashiriki na kuingia kiasi kikubwa cha fedha. Nimefarijika sana,” amesema Mwajeka.  “Mke wangu ni nesi, nilikuwa nachukua madaftari yake kuandika timu na kuanza kuzipigia mahesabu, nitatumia fedha hizi kwa ushauri wa wazazi wangu kuona ninafanya biashara gani,” amesema. Meneja Masoko wa Kampuni ya M-Bet, Allen Mushi Mushi amesema kuwa  M-Bet itaendelea kuwa nyumba ya mabingwa na kuwaomba mashabiki wa soka kubashiri na kampuni yao ili kuweza kubadili maisha. “M-Bet ni nyumba za mabingwa na mabingwa wote wanapatikana kupitia michezo ya kubahatisha ya kampuni yetu na kujitajirisha vile vile vile kuichangia nchi yao kwani asilimia 20 ya fedha hukatwa kama kodi ya kusaidia maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali,” amesema Mushi.
4
ZAIDI ya ekari 200,000 za ardhi kwa ajili ya malisho ya mifugo zimetengwa kwa wafugaji mbalimbali kupitia mpango wa matumizi ya ardhi, unaotekelezwa kwa pamoja kati ya taasisi za serikali na asasi za kijamii katika vijiji vya Alolle na Olengapa vilivyopo Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara.Taasisi zinazotarajia kutekeleza mradi huo ni Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC), Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Mifugo, na asasi ya kijamii ya KINNAPA na kuvihusisha vijiji vya Amei, Loolera, Lembapuli na Lesoit ambavyo kwa pamoja vinaunda jina la Alolle ikiwa ni muunganiko wa vijiji hivyo.Mafanikio hayo yameanza kupatikana hivi karibuni kupitia mradi wa uendelezaji endelevu wa sera na sheria ya ardhi ya Tanzania uliovisaidia vijiji husika kutumia kwa pamoja rasilimali hiyo ya ardhi na zingine zilizopo kwenye mipaka ya vijiji hivyo.Awali mradi huo ulisaidia kutenga ekari 75,000 za ardhi ya malisho katika eneo linalojulikana kama Olengapa, linalotumiwa kwa pamoja na vijiji vinne vya Orkitikiti, Lerug, Ngapapa na Engang’uengare vilivyopo katika eneo hilo la malisho katika wilaya hiyo Kiteto.
3
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limesema hatua ya serikali ya kurudisha kazi zote za chakula chini ya shirika hilo, limefanywa kwa wakati na tayari wameshaanza kupokea maombi mapya ya leseni na vibali vya chakula, kutoka kwa wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa hizo.Akizungumza kwenye Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabasaba, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile (pichani) alisema TBS imepokea majukumu hayo na tayari wameshaanza kuyatekeleza.Awali, masuala ya chakula yalikuwa wakifanywa kwa sehemu pia na iliyokuwa Mamlaka ya Dawa na Chakula na Dawa (TFDA), hivi sasa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA).“Unajua TBS sio kwamba tunapewa majukumu mapya kabisa, hapana tulikuwa tunafanya kwa sehemu yetu masuala ya chakula na mamlaka iliyokuwa ikishughulika na chakula na dawa nao walikuwa wanafanya kwa sehemu yao na tunazo mashine za kisasa za kupima vyakula na mambo mengine, sasa hili la kurudishwa kwetu moja kwa moja ni jema kwa sababu tuna uwezo nalo tangu mwanzo,” alisema Andusamile.Alisema kuanzia Julai mosi mwaka huu, walianza kupokea maombi ya vibali na leseni kutoka kwa wazalishaji, wasambazaji na wafanyabiashara wa vyakula kwa sababu leseni walizokuwa nazo awali ziliisha muda wake Juni 30, mwaka huu hivyo kutakiwa kisheria kuomba kuhuisha leseni zao au kuomba upya vibali na leseni.
5
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo juzi, Ibenge alisema kuwa wao hawatoibeza Mafunzo kwa kuwa wameifunga kwao mabao matatu bali wanachokitaka ni kuhakikisha mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo wakiwa nyumbani wanashinda.Alisema kuwa ushindi wao kwa mafunzo haukuwa rahisi hasa ukiangalia na mazingira ya mabao walivyoyapata ambapo mawili yote waliyafunga kwa adhabu hivyo ndani ya dakika 90 za mchezo wa marudio linaweza kutokea lolote.“Ushindi wetu haukuwa rahisi, tumepata mabao mawili yaliyotokana na adhabu hii inaonesha ni kwa kiasi gani wachezaji wa mafunzo walivyowazuri, kwa hivyo siwezi kuwabeza tutacheza kwa kujituma ili tupate ushindi,” alisema.Hata hivyo, alisema kuwa timu ya Mafunzo sio mbaya kihivyo, bali inahitaji kufanyiwa marekebisho madogo madogo ili iweze kuwa bora zaidi.Alisema kuwa kitu kikubwa ambacho amekigundua kwa timu ya Mafunzo ni wachezaji wake kukosa pumzi, jambo ambalo linahitaji kufanyiwa marekebisho.Kwa upande wake Mshauri wa Ufundi wa timu ya Mafunzo, Hemed Morocco alisema kuwa wamepoteza mchezo na wanajipanga kuhakikisha mchezo wa marudiano wanafanaya vizuri.Alisema kuwa kipindi cha kwanza cha mchezo huo vijana wake hawakucheza vizuri kutokana na timu kutojua mchezo wake hali ambayo ilitoa mwanya kwa wapinzani wao kuwafunga mabao hayo matatu ambayo yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza.“Wachezaji wangu hasa kipindi cha pili wamecheza vizuri na wapinzani wetu wametufunga kwa uzoefu, lakini kipindi cha pili vijana walicheza vizuri ingawa hawakufanikiwa kupata bao,” alisema.Hata hivyo alisema kuwa bado hawajakata tamaa na mchezo wao wa marudiano na matarajio yake makubwa ni kuona kuwa watafanya vizuri.
4
    Na Upendo Mosha – Moshi SIKU chache baada ya familia na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza kufanya shughuli ya kuuaga mwili wa kiongozi wa chama hicho, marehemu Philemon Ndesamburo katika viwanja vya Mashujaa mjini hapa, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imezuia. Badala yake, halmashauri hiyo imeelekeza Chadema kufanya shughuli hiyo katika Uwanja wa Majengo. Hoja za kuzuia uwanja huo ni pamoja na udogo, ikilinganishwa na idadi ya watu kutoka ndani na nje ya mji huo wanaotarajia kuhudhuria. Lakini pia kwa kuwa shughuli itafanyika siku ya kazi itasababisha usumbufu katika taasisi zilizo karibu na viwanja hivyo kama shule na mahakama. Zuio hilo limezua mtafaruku mkubwa kwa baadhi ya makada wa Chadema na wananchi waliokuwa katika eneo hilo kwa lengo la kufanya maandalizi ya kuaga mwili wa Ndesamburo ikiwamo kufanya usafi. Katika barua yake yenye kumbukumbu namba MMC/A.20/1/VOL.XV11/107 ya Mei 2, mwaka huu iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi, Patric Leyana, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imeeleza kuwa Chadema hawatakuwa na kibali cha kutumia uwanja huo kati ya Julai 5 hadi 6 kama walivyoomba “Inaonekana ni vema mkatumia Uwanja wa Majengo kufanya shughuli ya kumuaga marehemu kwa kuwa ni mkubwa zaidi na upo karibu na nyumbani kwa marehemu na uwanja una milango ya kutokea na kuingilia, hivyo itakuwa rahisi kuegesha magari,” ilieleza barua hiyo. Barua hiyo ya zuio iliwasilishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Wilaya ya Moshi, (OCD) Pankras Mdimi, ambaye aliisoma mbele ya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakiendelea na usafi katika viwanja vya Mashujaa na kisha kuwataka kuondoka mara moja katika eneo hilo. Akizungumzia zuio hilo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema lina sura ya kisiasa. Alisema shughuli ya umma ya kumuaga Ndesamburo hapo awali ilitangazwa kufanyika katika viwanja vya Mashujaa, ambavyo mara nyingi vimekuwa vikitumika katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiserikali, ikiwamo kampeni za ugombea wa urais.  “Eneo hili la Uwanja wa Mashujaa ni eneo lililopo katikati ya mji wa Moshi, sasa katika mazingira ya kushangaza kidogo wakati maandalizi yakiendelea, tulipata barua kutoka kwa mkurugenzi akielekeza kwamba kiwanja hicho hakitatolewa tena kwa ajili ya shughuli yetu,” alisema. Alisema Chadema haijashangazwa na kitendo cha kuhamishiwa Uwanja wa Majengo ila kinachowashangaza ni sababu za kipuuzi zilizotolewa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi.  “Sababu zilizotolewa na Mkurugenzi ni sababu za kitoto na kijinga sana, eti wanadai siku ya shughuli yetu ni siku ya kazi na mahakama itakuwa inaendelea  pamoja na shule, naziita ni za kijinga kwa sababu mahakama imekuwemo eneo hilo hata kabla ya uhuru na mikutano mbalimbali imekuwa ikiendelea pale na mahakama imekuwa ikiendelea na kazi yake na sababu ya shule ni ya kijinga kwani shule zimefungwa,” alisema Mbowe. Aidha alisema eneo la Majengo walilohamishiwa pia kumekuwa na shughuli mbalimbali ambazo zimekuwa zikiendelea na kwamba kuna hospitali, shule na makazi ya watu.  “Uwanja wa Majengo umepakana na Shule ya Sekondari Majengo na msingi pamoja na Hospitali ya Majengo. Swali je, hizo hazitasumbuliwa? Hivyo tunaona sababu hizo hazina mashiko,” alisema.  Alisema Chadema walitegemea kuwa viongozi wa Serikali wangetumia busara katika kushauriana suala hilo na si kufanya ubabe kama walivyofanya jambo ambalo alidai ni dhahiri lilikuwa halina nia njema na ni la kisiasa zaidi. “Polisi walianza kuzunguka uwanja na kuwataka watu waondoke, sasa jambo hili lilikuwa halina nia njema na limekaa kisiasa na ni dhahiri kwamba Serikali inatia doa zoezi la kumuaga mzee wetu na shujaa wetu Ndesamburo,” alisema Mbowe.  Alisema mbali na hayo, viongozi wa Chadema na familia ya Ndesamburo wamekaa na kujadiliana kwa kina ni wapi mahala sahihi pa kufanyia shughuli na kufikia uamuzi na kukubali kuhamia Uwanja wa Majengo. Awali wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya makada wa Chadema walionekana kuwa tayari kutokubali kuhamisha shughuli katika uwanja huo. Mbunge wa Moshi Vijijini, Anthony Komu, alisema wakiwa katika maandalizi ya kufanya usafi katika Uwanja wa Mashujaa, alifika OCD ambaye alidai kuwa ana maelekezo ya kuzuia maandalizi hayo.  “Yeye OCD amekuwa hapa akidai kuwa ana maelekezo kwamba tuondoke hapa na kwamba Mkurugenzi wa Manispaa anafanya utaratibu mwingine wa kutuhamishia Uwanja wa Majengo,” alisema.  Komu alishangaa zuio hilo kufanywa kwa Ndesamburo ilihali uwanja huo wa Mashujaa umekuwa ukitumika kufanya shughuli mbalimbali, ikiwamo mikutano ya dini hata katika siku za kazi.  “Huu ni msiba na msiba ni jambo ambalo halina itikadi na sioni sababu kubwa hasa ya kutuzuia na jambo hili, huu ni utamaduni mpya kabisa hapa kwetu, jambo hili halikubaliki,” alisema Komu. Alisema polisi ni vema wakafahamu kazi yao kubwa ni kulinda amani na kulinda shughuli hiyo iende kwa amani kwani Ndesamburo alikuwa ni kongozi aliyewahi kuendesha halmashaui hiyo kwa miaka zaidi ya 15 kwa amani. Aliba Bananga ambaye ni Diwani wa Kata ya Sombetini katika Jiji Arusha, alisema wao hawapo tayari kuondoka katika eneo hilo na kwamba ni vyema Serikali na Jeshi la Polisi wakaacha shughuli hiyo ifanyike kwa amani pasipo umwagaji wa damu.  Naye Elga Mchovu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) Mkoa wa Kilimanjaro, alisema wametumia gharama kubwa kusafisha uwanja huo, lakini anashangazwa na hatua ya Serikali ya kuwazuia licha ya taratibu nyingine kufuatwa. RPC AZUNGUMZA Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamisi Isah, alikiri polisi kuzuia shughuli hiyo kwa madai kuwa Chadema tayari walikwisha elekezwa kufanya shughuli hiyo Uwanja wa Majengo kwa kuwa kuna nafasi kubwa.
3
SIMBA inatarajia kutumia jezi za rangi ya kijivu kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Crescentius Magori alisema wamelazimika kutangaza rangi ya jezi hiyo mpya kutimiza matakwa waliyopewa na Shirikisho la Soka Afrika, CAF, kuwataka kuwa na jezi za aina tofauti baada ya kufika hatua ya robo fainali kwenye ligi hiyo msimu uliopita.Simba huvaa jezi nyekundu kwenye mechi za nyumbani na nyeupe kwenye mechi za ugenini, hilo limekuwa kwa muda mrefu kwa michuano mbalimbali. “Ilizoeleka Simba walikuwa na jezi aina mbili, rangi nyekundu na nyeupe ambazo zilikuwa zinavaliwa nyumbani na ugenini. Kwa muktadha huo timu ya Simba kwa sasa itakuwa na jezi aina ya tatu tukiongeza na jezi rangi ya kijivu na hili tumetimiza taratibu tulizopewa na CAF, kutaka kila timu iliyofika hatua hiyo kuwa na jezi ‘nyutro’ ambayo itavaliwa kwenye michuano hiyo kwa msimu unaokuja,” alisema Magori.Katika hatua nyingine, Magori alisema wamempeleka mwanachama wa timu hiyo Hamisi Kilomoni kwenye kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Soka nchini, TFF, ili wamchukulie hatua za kinidhamu kutokana na kuendelea kujitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa yeye ni mdhamini wa klabu hiyo ilihali anajua si kweli.“Sisi kama uongozi wa Simba tumeazimia kumpeleka kwenye kamati ya nidhamu ya TFF ashughulikiwe ili sisi tuende kutolea ushahidi na haki itendeke kwa sababu Simba kampuni hatuna kamati ya nidhamu kama tukiunda itaonekana tumefanya hivi kwa lengo la kumkomoa yeye,” alisema.Alisema Kilomoni alishatolewa kwenye udhamini kwa muda mrefu na sasa inafahamika wazi wanaoshika nafasi hiyo ni Abdu Abbas, Ramesh Patel, Profesa Juma Kapuya na Adam Mgoyi ambao wanafahamika kwa mujibu wa taratibu za kisheria za nchi. Aidha, Magori amebainisha kwamba wiki ya Simba day moja ya mambo watakayoyafanya ni kwenda kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa uwanja wa Bunju.
4
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Amiri Jeshi Mkuu  Rais Dk. John Magufuli, amepiga marufuku uuza uuzwaji wa sare za majeshi nchini na watu binafsi na kutaka wale wote wanaouza wazikabidhi kwa majeshi husika mara moja. Taarifa iliyotolea kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Jaffar Haniu ilisema Rais Dk. Magufuli alifia uamuzi huo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Gereza la Ukonga,Dar es Salaam. Taarifa hiyo, ilisema Rais Dk. Magufuli amepiga marufuku hiyo kutokana na maelezo ya baadhi ya askari wa Jeshi la Magereza kuwa wamekuwa wakinunua sare za jeshi hilo kutoka kwa watu binafsi kinyume na taratibu za majeshi. Kutokana na hali hiyo, Rais Dk. Magufuli ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwachukulia hatua mara moja wale wote watakaobainika kuuza sare hizo. ”Haiwezekani sare za majeshi yetu kuuzwa na watu binafsi hili haliwezekani kamwe, labda baada ya kumaliza muda wangu,” alisema Rais Dk. Magufuli” Pia amepiga marufuku majeshi yote  kuingia ubia na watu binafsi kupangisha ama kuuza maeneo yao kwa ajili ya kufanya biashara na kutaka maeneo ya majeshi yabaki katika jeshi husika. Katika hatua nyingine, Rais Dk. Magufuli ametoa Sh bilioni 10 kwa Jeshi la Magereza kwa ajili ya kujenga nyumba mpya zitakazotumika kwa ajili ya makazi ya askari wake katika Gereza la Ukonga. Hatua hiyo inatokana na kilio cha askari Magereza, kuwa wengi wao wamekuwa wakiishi uraiani kitu ambacho ni tofauti na taratibu za majeshi  hata kuzorotesha utendaji kazi wao wa kila siku. Taraifa hiyo, iliongeza kuwa ameagiza Jeshi la Magereza kuhakikisha wafungwa wanatumika ipasavyo katika uzalishaji mali,badala ya mfumo wa sasa ambapo baadhi wamekuwa  wakitutumia rasilimali za serikali bila kuzifanyia kazi. Aliwahakikishia  maofisa na askari wa  jeshi hilo kuwa Serikali itaendelea kuboresha maslahi yao na vitendea kazi kama inavyofanya kwa majeshi mengine.
3
Baraka juu ya baraka ehe! Ebwana eh! Mambo yanaizdi kumnyookea kijana wa Sultan na hasa baada ya kutoa series yake ya “Nakupenda mpaka kufa” na kinachotrend hivi sasa ni komenti ya  Madame Wema Sepetu akimtaka Idris  kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Siku ya leo Idris Sultan alipost picha akiwa yeye na Wema Sepetu na kuweka caption huku akimtag Wema Sepetu kwa kuwauliza mashabiki zake kama wakifanya filamu pamoja itanoga. Idris aliandika; Tukiwa movie moja itakuwa tatizo 😈🔥 @wemasepetu . . Plus sio kitambi, ni suti imevutwa nyuma na bidada Wema nae bila hila alishuka na bonge la komenti akigusia juu ya utani aliouweka Idris kwenye caption hiyo juu ya kuvutwa koti na kumalizia kumjibu juu ya uwezekano ya wawili hao kufanya filamu kwa pamoja na kumtaka wawe kwanza kimapenzi ndo mzigo uwe mkubwa. Idirs nae alireply kwenye komenti hiyo na kuandika; Idris na Wema Sepetu inasemekana walishawahi kuwa kimapenzi baada ya mara ya mwisho Wema kuachana na Diamond, penzi lao lilidumu kwa muda kadhaa kabla ya kuanguka kifo cha mende. Hili halikuonekana sana kuwakera mashabiki wao kwani wengi walioshuka kwenye uwanja wa comment wakiwa peace sana na wengine wakiwataka wawili hao warejee na wafanye kitu kikubwa.   Tukiwa movie moja itakuwa tatizo 😈🔥 @wemasepetu . . Plus sio kitambi, ni suti imevutwa nyuma na bidada . . 📸: @yuzo_mnene . “Nakupenda Kufa” episode mpya ipo kwenye app ya @mptv_tz A post shared by Idris Sultan (@idrissultan) on Feb 23, 2020 at 10:43pm PST
1
KLABU ya Simba ya Dar es Salaam imesema itafanya usajili wa kishindo kwa ajili ya msimu wa Ligi Kuu Bara 2018/19.Akizungumza kwenye tuzo za Mo Simba Dar es Salaam, Kaimu rais wa Simba, Salim Abdallah ‘Tray Again’ alisema mwekezaji wao amemwambia yuko tayari kumsajili mchezaji yeyote Afrika.“Simba inakwenda kusajili kwa kishindo, mwekezaji ameniambia yupo tayari kumsajili mchezaji yeyote Afrika, kwa hiyo tuna matumaini ya kufanya vizuri zaidi msimu ujao,” alisema.Simba ipo kwenye hatua za mwisho za kubadili mfumo wa uendeshaji kuingia kwenye utaratibu wa hisa ambapo mfanyabiashara na mwanachama wa klabu hiyo Mohamed ‘Mo’ Dewji ndiye mnunuzi wa hizo asilimia 49 dhidi ya 51 za wanachama.Mpaka sasa Simba haijaanza kufanya usajili wa wachezaji wa kimataifa, imesajili wachezaji wawili wa ndani na kumuacha wa kimataifa mmoja, Laudit Mavugo aliyemaliza mkataba wake.Aidha, Salim aliwapongeza wachezaji wake kwa kupambana kutwaa taji la Ligi Kuu na kwamba kupoteza mechi ya fainali dhidi ya Gor Mahia kwenye fainali za SportPesa Super Cup wiki iliyopita ni jambo la mpira.“Hongera kwa wachezaji mmepambana na kutwaa taji la Ligi Kuu, kwa bahati nzuri pia tumefika fainali za SportsPesa lakini kwa bahati mbaya tumepoteza, hiyo ndio soka… mpambane msikate tamaa,” alisema.
4
KLABU ya Real Madrid imeipiku Manchester United kwa thamani katika klabu za soka barani Ulaya, ikiwa na thamani ya karibu kiasi cha pauni bilioni 2.9 (sawa na Sh 8.706 trilioni),imeeleza Kampuni ya ukaguzi wa hesabu ya KPMG.Klabu hiyo ya Hispania licha ya kumaliza ya tatu katika msimu huu wa Ligi Kuu ya La Liga, tafiti za KPMG zimesema. Ripoti hiyo ya msimu wa mwaka 2016-17 na 2017-18, inatokana na faida ya haki za matangazo, umaarufu na thamani ya uwanja. Liverpool ambayo itacheza fainali dhidi ya Spurs wako katika nafasi ya saba na tisa katika viwango hivyo vya ubora.Huku Chelsea na Arsenal, ambao jana walitarajia kucheza fainali ya Ligi ya Ulaya wako katika nafasi ya sita na nane. Mabingwa wa Ligi Kuu ya England pamoja na Kombe la FA, wenyewe wako katika nafasi ya tano ikikamilisha jumla ya klabu sita za Uingereza kuwemo katika 10 bora. Real Madrid ilitwaa taji la Ligi ya Mabingwa katika misimu miwili, ambayo takwimu hizo zilichukuliwa, na kuongeza thamani yake kwa asilimia 10.Celtic iliyoshinda mara tatu taji la Scotland wenye wamo katika klabu 32 kubwa, ikiwa ni klabu ya kwanza kutoka nchini humo kuwemo katika orodha hiyo. Kiongozi wa KPMG, ambayo ni Kampuni ya Kimataifa, Andrea Sartori alisema kuwa jumla ya thamani yote imeongezeka kwa asilimia 9 kwa mwaka jana.Klabu 10 zenye thamani zaidi duniani: Real Madrid – Euro 3.224bn Manchester United – Euro 3.207bn Bayern Munich – Euro 2.696bn Barcelona – Euro 2.676bn Manchester City – Euro 2.460bn Chelsea – Euro 2.227bn Liverpool – Euro 2.095bn Arsenal – Euro 2.008bn Tottenham – Euro 1.697bn Juventus – Euro 1.548bn Chanzo: KPMG Sartori aliongeza: “Katika kiwango cha ligi,Ligi Kuu ya England imethibitisha kuwa ndio yenye thamani kubwa, ikiwa na klabu tisa katika klabu 32 za juu ikiwa na thamani ya asilimia 43 ya thamani yote.”Klabu nyingine za Uingereza zilizopo nje ya 10 bora ni West Ham United, Leicester City na Everton. Wakati huohuo, Inter Milan (iko katika nafasi ya 15) imepanda hadi katika nafasi ya tano na kuwa klabu yenye thamani zaidi nchini Italia,shukrani kwa kuongezeka kwa asilimia 41.
4
MIMBA katika umri mdogo ni miongoni mwa sababu zinazofi fi sha jitihada za kupunguza vifo vya akinamama na watoto hapa nchini.Kwa mujibu wa Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa, Rhobi Maro alisema wilaya hiyo ni miongoni mwa wilaya zinazokabiliwa na tatizo la mimba katika umri mdogo na ndoa za utotoni unaoweza kusababisha vifo kwa akina mama na watoto pindi wanapojifungua.Maro alisema serikali ya awamu ya tano imeweka miongozo mbalimbali ya kisera na kimkakati inayolenga kutokomeza vifo vya akinamama na watoto kwa kuboresha huduma za afya, hasa vijijini kwa kujenga vituo vya afya na vyenye uwezo wa kuweza kufanya upasuaji wa haraka ili kuweza kuokoa vifo vya akina mama na watoto.Aidha alisema kanuni za afya zinamtaka mwanamke kupata ujauzito wa kwanza akiwa amefikisha umri wa miaka 18, lakini hali haiko hivyo, watoto wenye miaka 14-17 wanajikuta wanabeba ujauzito kitu kinachotishia afya zao.“Sheria ya mtoto ya mwaka 2019 inasema mtu aliye chini ya miaka 18 ni mtoto hivyo anatakiwa kuwa chini ya uangalizi wa mzazi au mlezi hivyo mtoto huyo akipewa majukumu ya uangalizi kwa mtoto mwenzie inakuwa ngumu, lakini pia via vya uzazi vinakuwa bado havijawa tayari kuzalisha na hivyo vinaweza kusababisha vifo pamoja na ugonjwa wa fistula,” alisema Maro.Pia Maro alisema kuanzia mwaka 2013-2017 jumla ya watoto 11,880 walijifungua katika umri mdogo, kitu alichosema kinaashiria ukubwa wa tatizo katika wilaya hiyo.Kwa upande wake, Ofisa Mradi wa Shirika la Utu Mtoto, Clara Wisiko kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika hilo walibaini kuwa kati ya wenye miaka 13 hadi 17 watoto 3 kati ya watoto 10 tayari wameshapata mimba na wako katika malezi ya kulea watoto wenzao kitu alichosema kinafifisha ndoto nyingi za wasichana hao na kujikuta katika lindi kubwa la umaskini.Clara Wisiko alisema kuwa chanzo kikubwa cha mimba za utotoni katika kata wanazofanya nazo kazi ni maskini wa kipato kwa wazazi, umbali wa huduma za jamii, kama maji, upatikanaji wa kuni pamoja umbali kati ya shule na vilipo vitongoji na vijiji wanapoishi wazazi wa watoto hao.Wisiko alisema utafiti huo uliofanywa katika kata nne za Kibakwe, Mpwapwa mjini, Berege na Pwaga, uligundua kuwa watoto wengi walio chini ya miaka kumi na sita wamejikuta wakiingia katika malezi na hivyo wengi wao kuathirika kisaikolojia na hivyo kushidwa kuwa wazalishaji na kubaki kuwa tegemezi.Wisiko alisema sababu nyingine ni ukosefu wa elimu ya uzazi kwa watoto wa kike, unachangia kwa kiasi kikubwa cha upatikanaji wa mimba za utotoni ambapo mtoto hulazimka kudanganywa na mtu mzima na kupewa kitu kidogo ili aweze kukidhi mahitaji yake yanayomkabili kwa wakati ule.Hata hivyo Wisiko alisema kwamba pamoja na kuwapo kwa miongozo, sera na sheria ya mtoto lakini bado kuna vitendo vya ukatili dhidi ya mtoto kutokana na usimamizi hafifu wa miongozo hiyo au kutokufahamika kwa wadau dhidi ya kuchukua hatua kwa ajili ya mstakabali wa mtoto.Alisema kuwa shirika hilo limelenga kushirikisha jamii na serikali kukabili changamoto hizo kwa kufanya utafiti shirikishi ambao hushirikisha jamii yenyewe kutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo.
3
Katika mitandao ya kijamii huko kumechafuka baada ya mwanamuziki wa bongo fleva Dullahmakabila kuposti picha katika mitandao ya kijamii akijigeuza kuwa mwanamke. Katika picha hizo Dulla ambaye mwonekano wake halisi ni huo hapo juu amejiremba misiri ya mwanamke na wale wazee wa kuzama DM wanaweza wakajichanganya wasipousoma vizuri mchezo. Hata hivyo mashabiki zaidi ya 1,200 walikomenti katika posti yake ya kwanza ya aina hiyo wengi wamemshambuliwa kuwa anawadhalilisha wanaume huku wengine wakimpiga kwa dini yake wakisema kuwa kama Mwisilamu hapaswi kufanya hivyo. Makeup By @zuhuraty_beautymakeup Shot | Retouching And Colour By @20r_touchez. . I #NingekuwaDemuIngekuaje ? A post shared by MAKABILA (@dullamakabila) on Feb 10, 2020 at 12:38am PST Wapo waliomfananisha na staa mwanamke katika muziki wa bongo fleva Luludiva na wengine wakimfananisha na Mama Dangote. Kumbe yote ya yote dogo alikuwa anatafuta kiki bana ya kutoa wimbo wake uitwao kama ningekuwa mwanamke. Madanga Yangenikoma Kama Ningekuwa Demu, Maana Mi Na Bwana Angu Mwiko Ungekuwa Kulala 😋😊 LINK KWA BIO. . #NingekuwaDemu Art By @mariot_alvero A post shared by MAKABILA (@dullamakabila) on Feb 10, 2020 at 5:14am PST
1
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu (pichani) alisema hayo jana wakati alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu athari za umeme katika sekta ya viwanda. Alisema wizara yake haifurahishwi na tatizo la nishati nchini na imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi, hali ambayo pamoja na kuwasaidia kimaisha Watanzania lakini pia itasaidia uzalishaji wenye tija viwandani. “Wizara kwa kweli haifurahii kabisa tatizo hili la kupanda kwa bei ya umeme kwa kuwa lazima itaathiri gharama za uzalishaji, kupanda kwa bei za bidhaa na kupunguza uwezo wa uzalishaji viwandani na hivyo kupunguza ajira jambo ambalo linaenda kinyume kabisa na mpango wa Serikali,” alisema Nyalandu. Alisema pamoja na hayo, juhudi zinafanyika kuhakikisha Tanzania inakuwa na umeme wa uhakika na wenye gharama nafuu ili kuwezesha uzalishaji wa bidhaa kwa kiwango cha juu na ziuzwe kwa bei nafuu. Wiki iliyopita Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ilitangaza kuanza kwa bei mpya ambazo ni ongezeko la asilimia 40.29 zilizoanza kutumika rasmi jana hali ambayo ilipokewa kwa hisia tofauti na watumiaji wengi wakiwa na hofu ya maisha kuzidi kupanda.
5
KHARTOUM, SUDAN RAIS wa Sudan Omar al-Bashir amekiri kuwa madai ya waandamanaji wanaoipinga serikali ni halali isipokuwa tu yalifanyika kinyume cha sheria na kusababisha vifo vya watu kadhaa. Akizungumza katika hotuba yake ya kwanza Bungeni tangu kutangazwa kwa hali ya dharura Februari 22 mwaka huu, Bashir amesema mgogoro wa kiuchumi umeathiri sehemu kubwa ya raia. Alisema kutokana na hali hiyo, raia walikuwa na haki ya kuandamana kueleza machungu yao. Lakini aliongeza kuwa tatizo ni namna yalivyoendeshwa, baadhi waliingia mitaani kuelezea matakwa yao ya halali, lakini wengine waliokusanyika walitumia njia haramu kuharibu mali. Katika siku za mwanzo za maandamano hayo yaliyoanza Desemba 19, ofisi kadhaa na majengo ya chama tawala cha Bashir vilichomwa moto. Maafisa wanasema watu 31 wameuawa mpaka sasa katika maandamano hayo, huku Shirika la Haki za Binadamu (HRW) likisema idadi ya vifo ni 51. Bashir mwenye umri wa miaka 75 ambaye aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi mwaka 1989, awali alitangaza hali ya dharura kwa mwaka mmoja lakini bunge liliipunguza hadi miezi sita.
2
BAADA ya kukabidhiwa rasmi na serikali ndege aina ya Fokker 50, Kampuni ya Ndege nchini (ATCL) imesema itaiingiza ndege hiyo katika ratiba yake ya safari za ndani ya nchi. Miongoni mwa safari hizo za ndani ni pamoja na ya Mtwara ambayo itaanza Machi 15 mwaka huu pamoja na ya Iringa, inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa ATCL, Josephat Kagirwa, aliliambia HabariLeo jana kuwa ndege hiyo ya Fokker 50 itakuwa msaada mkubwa katika kusafirisha abiria wachache wanaofikia 44, hivyo kuokoa mafuta na muda kama ndege kubwa zaidi ya hiyo, ingetumika kusafirisha abiria wachache. Mbali na kusafiri kwenda Mtwara na Iringa, ndege hiyo pia kama ilivyo kwa ndege zingine za Bombardier Dash 8 Q400 na Airbus A220-300, itakuwa ikifanya safari katika mikoa ya Kigoma, Kilimanjaro, Tabora, Mwanza, Mbeya na Zanzibar.“Ujio wa ndege hii, utasaidia kutoa huduma katika masafa mafupi, kusafirisha abiria wachache ili kuokoa mafuta tofauti kama ingetumika ndege kubwa ya abiria 70 kusafirisha abiria 40,”alieleza Kagirwa. Kuhusu ndege za ATCL kuanza safari za China, India, Thailand na Afrika Kusini, alisema kuwa maandalizi ya safari hizo yamefikia asilimia 75 mpaka sasa.Alisema kwa kuwa kutoka Dar es Salaam hadi India, inachukua muda wa saa tano na kwa kuwa ndege ya Airbus 220-300 ina uwezo wa kufanya safari za masafa ya kati, zinazochukua muda kati ya saa sita hadi saa sita na nusu, hivyo inaweza kuungana na ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner kusafirisha abiria kwenda India na kurudi. Kagirwa alisema kwa safari za China na Thailand itakuwa ikienda Boeing 787- 8 Dreamliner pekee, kwa kuwa ina uwezo wa kufanya safari za masafa marefu kwa ndege hiyo ina uwezo wa kusafiri kwa muda wa saa 18 angani bila kutua mahali popote.Kukabidhiwa kwa ndege hiyo ya Fokker 50, inaifanya ATCL kuwa na jumla ya ndege saba ikiwemo Boeing 787-8 Dreamliner, ndege mbili za Airbus A220-300 na ndege tatu aina ya Bombardier Dash Q400. Rais Magufuli aliwahi kusema kuwa ndege nyingine ya pili aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, itawasili nchini mwishoni mwa mwaka huu na ndege nyingine ya nne aina ya Bombardier Dash 8 Q400, nayo itawasili mwishoni mwa mwaka huu au mwaka ujao mwanzoni.
3
RAIS John Magufuli amesema serikali itachukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) haifi wala haifanyi kazi chini ya kiwango.Alisema Mamlaka hiyo ni maono ya waasisi wa mataifa ya Tanzania na Zambia, Mwalimu Julius Nyerere na Kenneth Kaunda na walikuwa wameona mbali katika uchumi wa nchi hizi mbili hivyo mamlaka hiyo haiwezi kufa.Rais Magufuli aliyasema hayo jana katika Stesheni ya Tazara jijini Dar es Salaam kabla kuanza safari kwenda Kisaki mkoani Morogoro na baadaye Rufiji mkoani Pwani kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Mradi wa Kuzalisha Umeme katika Mto Rufiji.“Kwa hiyo ‘it will never die’ (kamwe halitakufa). Serikali inatambua umuhimu wa Tazara na haiwezi kuiacha ikafa au ikafanya kazi kwa ufanisi mdogo usiowaletea manufaa Watanzania kama ilivyokusudiwa,” alisema Rais Magufuli.Aliiagiza menejimenti ya shirika hilo kuwasilisha kwake mapendekezo yao juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa na serikali ili kuboresha usafirishaji wa abiria na mizigo kupitia Tazara.Alitoa maelekezo hayo muda mfupi baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Tazara, Bruno Chingandu na Meneja Mkuu wa Tazara Tanzania, Fuad Abdallah kumweleza kuwa tayari mapendekezo ya uboreshaji wa shirika hilo yamewasilishwa serikalini ili kuwezesha kila nchi kuwekeza katika shirika hilo kwa lengo la kuboresha usafirishaji wa abiria na mizigo.Aidha Rais Magufuli aliitaka menejimenti ya shirika hilo kuwasikiliza na kusaidia kutatua shida za wafanyakazi wake ili wafanye kazi kwa weledi na zitakazowashinda waziwasilishe serikalini.“Wafanyakazi inaonekana wana shida nawauliza maswali wanaogopa kujibu, lakini wanaonekana wana shida kibao, inaonekana mnawatisha wasiseme labda wakisema mnawafukuza kazi,” alisema Rais Magufuli.Tazara iliyojengwa kwa msaada kutoka China, ilianza kutoa huduma mwaka 1975 na inamilikiwa kwa ubia wa asilimia 50 kwa 50 wa nchi ya Tanzania na Zambia. Reli hiyo yenye urefu wa kilometa 1,860 ina uwezo wa kusafirisha tani milioni 5 za mizigo kwa mwaka, lakini kutokana na uwekezaji mdogo uliosababisha upungufu mkubwa wa injini na mabehewa inasafirisha chini ya tani 300,000 kwa mwaka.
3
WASHINGTON, MAREKANI RAIS wa Marekani Donald Trump, ametangaza kuweka zuio kwa raia wa nchi za Ulaya kuingia nchini Marekani ili kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona. Katika hotuba yake kwa njia ya Televisheni siku ya Jumatano, alisema safari zote za kutoka Ulaya zitazuiwa kwa siku 30 zijazo. Lakini amesema ”hatua kali zilizo na umuhimu” hazitaihusisha Uingereza, ambayo ina visa 460 vya virusi vilivyothibitishwa. Kuna visa 1,135 vilivyothibitishwa nchini Marekani na watu 38 wameripotiwa kupoteza maisha. ”Kuzuia visa vipya kuingia Marekani, tutaahirisha safari zote kutoka Ulaya,” Trump alieleza. ”Hatua hii itaanza kutekelezwa kuanzia usiku wa siku ya Ijumaa”. Aliongeza. Trump amesema Umoja wa Ulaya umeshindwa kuchukua hatua za tahadhari kama hizo zilizoanzishwa na Marekani. Alizungumza saa kadhaa baada ya Italia nchi iliyoathirika zaidi baada ya China kutangaza kuchukua hatua kali. Hatua hizo ni pamoja na kufunga maduka yote isipokuwa yanayouza vyakula na dawa kama sehemu ya kujitenga. Trump amesema kuahirishwa kwa safari pia kutahusu biashara na usafirishaji wa mizigo kutoka Ulaya kuingia Marekani. Pia ametangaza kutoa mkopo wa mabilioni ya dola kwa wafanyabiashara wadogo, na kutaka bunge la Congress kupitisha nafuu ya kodi ili kukabiliana na athari za mlipuko wa corona kiuchumi. HALI ILIVYO MAREKANI Maofisa wamesema hatari ya maambukizi ilikuwa chini, lakini hali ilibadilika baada ya ongezeko la idadi ya visa vipya vya maambukizi vilivyothibitishwa mwanzoni mwa mwezi Machi. Jitihada za kudhibiti zimeanza. Vikosi vimepelekwa kwenye mji wa New Rochelle, ulio kaskazini mwa New York, ambapo mlipuko huo unaaminika kuanzia huko. Vikosi vya ulinzi vitatoa chakula kwa baadhi ya watu ambao wametakiwa kujiweka karantini. Gavana wa jimbo la Washington amepiga marufuku mikusanyiko katika kaunti kadhaa. Jimbo lililo Kaskazini Magharibi ni kiini cha maambukizi nchini Marekani, kukiwa na idadi ya vifo 24 kati ya 38 nchi nzima. Mkuu Shirika la Afya Duninai (WHO), Dk. Tedros Adhanom Ghebreyes ametangaza mlipuko wa Corona kuwa janga la kimataifa Shirika la Afya duniani limeutangaza mlipuko wa virusi vya corona kuwa ni janga la kimataifa, huku mlipuko huo ukiendelea kusambaa katika mataifa mbalimbali duniani. Ghebreyesus amesema kuwa idadi ya visa nje ya China vimeongezeka mara 13 kwa kipindi cha majuma mawili yaliyopita. Amesema kuwa ana hofu kubwa kutokana na viwango vya maambukizi ya virusi. Janga ni ugonjwa ambao unasambaa katika nchi nyingi kote duniani kwa wakati mmoja. ITALIA Waziri Mkuu, Giuseppe Conte alitangaza ongezeko la masharti ya kujiweka karantini kuongezeka. Alisema maduka mengi, migahawa, saluni, vitafungwa hadi Machi 25. Italia ina watu 12,000 waliothibitika kuambukizwa na idadi ya waliopoteza maisha ni 827. Karibu watu 900 wenye maambukizi wako kwenye hali mbaya, WHO imesema. Wakati huo huo Saudi Arabia imesitisha kwa muda usafiri wa raia wake na wakaazi wengine na kuzuia safari za ndege kwenda katika mataifa kadhaa kutokana na hofu ya virusi vya Corona. Shirika la habari la nchi hiyo SPA lilisema jana na kutaja chanzo rasmi katika wizara ya mambo ya ndani. Uamuzi huo unajumuisha mataifa ya Umoja wa Ulaya, Uswisi, India, Pakistan, Sri Lanka, Ufilipino, Sudan, Ethiopia, Sudan Kusini Eritrea, Kenya, Djibouti na Somalia, chanzo hicho kimeongeza, kikisema Uingereza pia imesitisha kuingia nchini humo kwa wale watu wanakuja kutoka nchi hizo. Saudi Arabia pia imesitisha kwa muda usafiri wa abiria na pia kwa njia ya barabara na Jordan, wakati usafirishaji wa mizigo na biashara vinaruhusiwa bado, na usafirishaji wa abiria wenye uhitaji maalum wa kiutu.
2
Matawi hayo yamefanya sasa benki hiyo kuwa na matawi 24 katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mara, Mwanza, Geita na Kagera. Kwa upande wa nchi nzima, benki hiyo sasa imefikisha matawi 176 na mashine za kutolea fedha (ATM) zaidi ya 600.Matawi hayo mapya ya Nyamongo na Katoro kwa pamoja yanahudumia Watanzania zaidi ya 600 kila siku, hatua ambayo imetajwa kuwa imewapunguzia wananchi wa maeneo hayo adha ya kufuata huduma mbali.Akizungumza katika ufunguzi matawi haya, Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, Abraham Augustino alisema lengo kubwa la kupeleka matawi hayo ni kuwapa huduma kwa ukaribu wateja wao waliopo katika maeneo hayo husika.Alifafanua kwamba, tangu kuanzishwa kwa matawi hayo yamekuwa ni mkombozi kwa wateja wengi wakiwemo wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na watu mbalimbali. “Wakazi wa Nyamongo walikuwa wanasafiri mpaka Tarime kupata huduma za kibenki huku wale wa Katoro mpaka waende Geita ambapo ndiko kulikokuwa na matawi ya benki,” alisema Augustino.Maeneo yote haya yanakaliwa na wafanyabiashara zaidi na wavuvi ambao huduma za kibenki kwao limekuwa ni jambo muhimu ili kuondoa uwezekano wa kutunza fedha majumbani, hivyo kuhatarisha maisha yao kutokana na ujambazi.
5
Mwandishi Wetu – Dar es Salaam TANZANIA imewaahidi wajumbe wa kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UN), kuwa itafanya uchaguzi huru na haki kwa mujibu wa sheria. Pamoja na hali hiyo, imesema kuwa hatua zote ambazo zimechukuliwa na Bunge kwa kufanya mabadiliko katika sheria za vyama vya siasa, sheria ya mashirika yasiyo ya kiserikali na ile ya vyombo vya habari zina lengo la kuimarisha uwajibikaji na uwazi pamoja na kuhakikisha misingi na tunu za taifa zinaheshimiwa na kuendelezwa. Ahadi ya kufanyika kwa uchaguzi huru na wa haki sasa imevuka nje ya mipaka ya Tanzania ambapo kwa mara ya kwanza, ilitolewa na Rais Dk. John Magufuli, Januari 21, mwaka huu alipokutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao  Tanzania katika sherehe za mwaka mpya 2020 na chakula cha jioni zilizofanyika Ikulu, Dar es Salaam. Rais Magufuli alisema kuwa utakapofika uchaguzi, nchi na taasisi mbalimbali zitakaribishwa Tanzania kushuhudia. Akihutubia jana katika kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UN), linaloendelea Geneva nchini Uswisi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, aliihakikishia Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania inaheshimu na itaendelea kuheshimu haki zote za binadamu zikiwemo za kisiasa. Alisema sheria zilizotungwa na Bunge zina lengo jema la kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa taifa lenye amani, umoja na utulivu. Profesa Kabudi alisema kuwa mwaka huu Tanzania itafanya Uchaguzi Mkuu wa sita tangu kuanzishwa kwa vyama vingi vya siasa na kuihakikishia jumuiya hiyo kuwa uchaguzi huo utakuwa wa uwazi, huru na wa haki. Alisema kuwa waangalizi mbalimbali wa uchaguzi wa ndani na nje ya nchi watakaotaka kushuhudia namna Watanzania wanavyotekeleza moja ya haki zao za msingi katika suala la kidemokrasia  kwa kuchagua viongozi wao. “Tanzania inaheshimu na itaendelea kutekeleza kwa vitendo haki zote za binadamu bila ubaguzi, na kwamba madai yanayoishutumu Tanzania kukiuka haki za binadamu ni propaganda na hasa zinatokana na hatua kali zinazochukuliwa dhidi ya rushwa, ubadhirifu wa mali za umma, madawa ya kulevya, uzembe katika ofisi za umma pamoja na hatua zinazochukuliwa kulinda rasilimali na maliasili ya Tanzania kwa manufaa ya Watanzania,” alisema Profesa Kabudi. Akizungumza kuhusu masuala ya sheria mpya za huduma vyombo vya habari na haki ya kupata taarifa, Profesa Kabudi aliiambia jumuiya ya kimataifa kwamba sheria hizo zilizotungwa na Bunge zina lengo la kuimarisha, kulinda na kuweka mazingira bora zaidi kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa usalama na kwa kuzingatia taaluma sambamba na kuwawezesha kupata haki zao ikiwa ni pamoja na mishahara bora na mikataba ya kazi. MAREKANI YAPONGEZA Siku chache baada ya kauli ya Rais Magufuli, kuahidi uchaguzi huru na wa haki, Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ulimpongeza Rais Magufuli baada ya kiongozi mkuu huyo wa nchi kueleza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2020 utakuwa huru na haki. Mbali na pongezi hizo, ubalozi huo ulitaka kuharakishwa kwa uanzishwaji wa tume huru ya uchaguzi. Januari 21, mwaka huu Rais Magufuli aliwahakikishia mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania kuwa uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki, ambapo kauli hiyo iliibua mjadala miongoni mwa vyama vya siasa na wanaharakati wa demokrasia wakihoji uwezekano huo bila kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi. Katika taarifa ya ubalozi huo iliyotolewa Januari 31, mwaka huu ubalozi huo umeonyesha kutiwa moyo na kauli ya kiongozi mkuu huyo wa nchi. “Tunatoa wito wa kuharakishwa kwa zoezi la uandikishaji wapigakura lenye uwazi, kuanzishwa kwa tume huru ya uchaguzi na kuteuliwa mapema kwa waangalizi wa uchaguzi wa kitaifa na wa kimataifa wa kuaminika watakaofuatilia uchaguzi kwa kipindi kirefu na kipindi kifupi,” ilieleza taarifa hiyo. KABUDI NA JUMUIYA YA MADOLA Katika tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Kabudi, alikutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Patricia Scotland mazungumzo yaliyolenga masuala kadhaa, ikiwa ni pamoja na mradi ambao Jumuiya ya Madola umeufanya kuhusu Tanzania. Mradi huo umelenga kuangalia takwimu mbalimbali zinazohusu biashara kwa kuangalia nchi ambazo Tanzania inaagiza ama kuuza bidhaa zake kwa wingi katika nchi za Jumuiya ya Madola mradi ambao umeelezwa kuwa na manufaa makubwa kwa nchi ambapo kwa sasa nchi za India na Afrika Kusini ndizo kinara. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Patricia, alisema Tanzania ni mdau muhimu katika jumuiya hiyo na kwamba amefurahi kumkabidhi Profesa Kabudi nakala ya utafiti huo kwa niaba ya Tanzania, jambo litakaloifanya kuendelea kuangalia maeneo ya kujiimarisha katika ufanyaji wa biashara na nchi za Jumuiya ya Madola. Mbali na masuala hayo ya mradi huo wa takwimu wa biashara kuhusu Tanzania uliofanywa bure na Jumuiya ya Madola, pia viongozi hao walizungumzia masuala mengine ikiwa ni pamoja na namna jumuiya hiyo na Tanzania zitakavyofanya kuongeza usawa wa jinsia, masuala ya haki za binadamu pamoja na uimarishaji wa mfumo wa mahakama nchini.
3
NAIBU Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kusitisha mpango wake wa kurasimisha bandari bubu zilizopo Mkoa wa Dar es Salaam.Nditiye aliyasema hayo wakati wa ziara yake wilayani Bagamoyo ya kukagua bandari bubu zilizopo. Alisema amebaini uwepo wa bandari bubu zaidi ya 19, zinazosafirisha bidhaa kwenye eneo la mwambao wa bahari lililopo wilayani humo.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, uwepo wa bandari bubu hizo ni kipenyo cha baadhi ya wafanyabiashara, kukwepa kulipa kodi kwa kutumia bandari rasmi na hivyo kupunguza mapato ya Serikali na kuihujumu nchi.Alisema uwepo wa bandari hizo, hufifisha jitihada za Serikali za kufikia uchumi wa kati na azma yake ya ujenzi wa viwanda, utoaji wa huduma za afya, elimu, maji, umeme na ujenzi wa miudombinu katika maeneo mbalimbali nchini.Nditiye aliielekeza TPA iache mara moja mpango huo wa kurasimisha bandari bubu zilizopo Mbweni na Temeke, kwa kuwa Dar es Salaam ipo bandari na itumike hiyo kwa shughuli za usafirishaji wa bidhaa na abiria.“TPA wafute mara moja mpango wao wa kurasimisha bandari bubu za Mbweni, Temeke kuwa bandari rasmi wakati kuna bandari ya Dar es Salaam... fedha zilizotengwa na TPA kwa ajili ya mpango huo lipewe jeshi la bandari ili waweze kununua vifaa kwa ajili ya kufanya doria ya kuimarisha ulinzi kwenye mwambao wa bandari,” alisema.Alisema yapo majahazi yanayofanya shughuli za usafirishaji ufukweni mwa Bahari ya Hindi kwenye mwambao wa kilomita 300 kwenye eneo la Bagamoyo. Alisema majahazi hayo yanashusha mizigo kinyemela.Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainab Kawawa alikiri uwepo wa bandari bubu zaidi ya 19 na alimweleza Nditiye kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto za uwepo wa bandari bubu. Kawawa alitaja baadhi ya bidhaa zinazovushwa kuwa ni sukari, mafuta ya kula, matairi ya magari, maziwa ya unga, vitenge, khanga na vipodozi pamoja na wahamiaji haramu.Alisema hadi sasa kuna wafungwa wapatao 203 waliopo gerezani kutokana na uwepo wa wahamiaji haramu. Alisema watumishi hao wanatumia bandari bubu zinazotokana na uwepo wa Bahari ya Hindi wilayani humo na alizitaja kuwa ni Mlingotini, Kasiki, Kaole, Magambani, Kilimani, Badeco, Msalabani, Nunge, Mtailindi, Jicho Kuu, Mto Ruvu, Razaba, Gama, Kayanjo – shamba la chumvi, Saadani, Kitongoji cha Gwaza, Changwahela na Duza.
3
  Na Tobias Nsungwe – Dar es Salaam BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeotoa ripoti ya hali ya uchumi inayoishia mwezi Machi, mwaka huu huku ikionyesha ongezeko kubwa la bei ya vyakula. Ripoti hiyo imeonyesha kupanda kwa mfumuko wa bei za vyakula kutoka asilimia 5.2 mwezi Januari hadi asilimia 5.5 Februari, mwaka huu. Kwamba hali hiyo imesababisha kupanda kwa bei za nafaka, hasa mahindi, unga wa mahindi, ndizi, maharage sambamba na vinywaji baridi. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kiwango cha mfumuko wa bei kwa mwaka kwa vyakula na vinywaji visivyo na kilevi ambazo ni bidhaa zinazokusanya walaji wengi zaidi, kilipanda zaidi ya kiwango cha kawaida cha mfumuko wa bei.  Kwa mtindo wa ripoti ya mwezi hadi mwezi, mfumuko wa bei ulikuwa ni ailimia moja kwa mwezi Februari mwaka huu, ikilinganishwa na asilimia 0.7 ya Februari mwaka jana. Taarifa ya BoT pia imesema kiwango cha kukua kwa mfumuko wa bei kwa vyakula na vinywaji visivyo na kileo ni asilimia 8.7 mwezi Februari toka asilimia 7.6 ya mwezi Januari mwaka huu. Kwa kufuata ripoti ya mwezi hadi mwezi, kiwango hicho kilikuwa ni asilimia 2.3 mwezi Februari mwaka huu, ukilinganisha na asilimia 1.2 mwezi Februari mwaka jana. Viwango vya mfumuko wa bei kwa vitu visivyo vyakula, ilikuwa ni asilimia 3.6 hadi mwisho wa mwezi Februari mwaka huu kama ilivyokuwa mwezi uliotangulia. Kwa msingi wa mwezi hadi mwezi, kiwango cha mfumuko wa bei kwa vitu visivyo vyakula ilikuwa ni asilimia 0.4 mwezi Februari mwaka huu kama ilivyokuwa mwezi kama huo mwaka jana. Mfumuko wa bei kwa nishati na mafuta kulipanda hadi asilimia 12.3 kufikia mwezi Februari mwaka huu toka asilimia 11.5 mwezi Januari mwaka huu.  Katika ripoti ya mwezi hadi mwezi, kiwango kilikuwa asilimia 2.1 mwezi Februari mwaka huu ukilinganisha na asilimia 1.4 mwezi Januari mwaka jana. Ripoti hiyo imesema pia kuwa katika ripoti ya miezi 12 ya mfumuko wa bei kwa bidhaa zote ukiacha chakula na nishati, ulipungua kwa asilimia 2.2 mwezi Februari mwaka huu kutoka asilimia 2.3 ya mwezi Januari mwaka huu. Kwa ripoti ya mwezi kwa mwezi, kiwango cha mfumuko wa bei kilikuwa ni asilimia 0.1 mwezi Februari mwaka huu ukilinganisha na asilimia 0.2 mwezi Februari mwaka jana. Ripoti ya BoT imekuja siku chache baada ya baadhi ya wabunge kulalamikia kuwapo kwa tishio la njaa nchini. Hali hiyo ilijitokeza bungeni wiki iliyopita wakati wabunge hao walipoanza kuomba mwongozo kwa Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson.
3
WATU 19 kati ya 27 waliokuwa wakishikiliwa na Polisi wakihusishwa na tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara bilionea nchini, Mohammed Dewji maarufu MO, wameachiwa kwa dhamana huku likiahidi mfanyabiashara huyo atapatikana.Akizungumza na gazeti hili, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alisema watuhumiwa hao wameachiwa baada ya mahojiano na timu ya wapelelezi wanaoshughulikia suala hilo wakati huu, ambao juhudi za kumtafuta bilionea huyo zikiendelea kufanywa na vyombo mbalimbali vya usalama.Dewji (43) alitekwa na watu wasiojulikana alfajiri ya Oktoba 11, mwaka huu katika Hoteli ya Colloseum, Oysterbay Dar es Salaam alipokuwa amekwenda kufanya mazoezi (gym) na kusababisha hali ya taharuki katika jamii ya kitaifa na kimataifa huku kukiwa hakuna taarifa zozote juu ya sababu za kutekwa kwake.Kutokana na tukio hiyo, familia ya mfanyabiashara huyo juzi ilijitokeza hadharani na kutangaza dau nono la Sh bilioni moja kwa mtu yeyote atakayesaidia kutoa taarifa zitakazosaidia kupatikana kwa bilionea huyo kijana.“Tumewaachia kwa dhamana watu 19 baada ya kuwahoji kwa kina kuhusu tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara huyo, huku tukiendelea kuwashikilia wengine saba wakati huu tunapoendelea kufanya upelelezi wetu dhidi ya tukio hilo,” alisema Kamanda Mambosasa.Aidha, alisema anaamini Mo Dewji atapatikana kutokana na jitihada zinazoendelea kufanyika huku akiomba ushirikiano kutoka kwa wananchi wote zitakazosaidia kufanikisha kupatikana kwake.Alisema Polisi inaendelea kutumia njia mbalimbali ili kuhakikisha anapatikana pamoja na kuwapata wahusika wa kitendo hicho ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake kutokana na tukio hilo. Akizungumza juzi kwa niaba ya familia ya mfanyabiashara huyo, Msemaji wa familia hiyo, Azim Dewji alisema familia hiyo imeamua kutangaza donge nono la fedha hizo kwa nia ya kuongeza nguvu ya utafutaji wa kijana wao.Alisema taarifa zozote zitakazotolewa zitakuwa za siri kubwa baina ya mtoa taarifa na familia hiyo, na kuishukuru serikali kwa jitihada kubwa wanazozifanya kuhakikisha mfanyabiashara huyo anapatikana.Alisema kwa yeyote mwenye taarifa hizo, awasiliane nao kupitia kwa Murtaza Dewji kwa namba 07550300 au 0717208478 au barua pepe findmo@melt.net Katika hatua nyingine, Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema amewataka waliomteka MO Dewji kumwachia huru, kwa kuwa wanamharibia Rais John Magufuli na Tanzania kwa ujumla.Akizungumza jana na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, Lema alibainisha kuwa tukio hilo sio zuri kwa taswira ya nchi, kwa kuwa linaweza kusababisha wafanyabiashara wakubwa kukimbia nchi.Alisema kwa miaka mitano aliyofanya kazi kwa ukaribu zaidi na MO Dewji alipokuwa Mbunge wa Singida Mjini, anamfahamu kuwa ni mtu asiye na makuu, licha ya utajiri mkubwa alionao.Aliwataka watekaji hao, kumwachia huru kwa kuwa ni mtu mzuri aliyekuwa akisaidia uchumi wa nchi, akibainisha kuwa Kampuni za Mohamed Enterprises zinachangia asilimia 3.5 kwenye Pato la Taifa na imeajiri watu zaidi ya 25,000.Aliongeza kwa kuwa Rais Magufuli tangu kuingia madarakani, amesaidia kukuza uchumi wa nchi hivyo kutekwa kwa bilionea huyo tajiri kutatoa taswira ya kuwa nchi sio salama. “Kutekwa kwa MO sio jambo dogo hata kidogo… huyu ni mfanyabiashara tajiri kijana Afrika, huenda pengine waliofanya hivi ni watu wenye nia ya kuhujumu uchumi wetu,” alisema Lema.Aliongeza, kutokana na unyeti wa tukio hilo ni vema serikali kuwashirikisha wachunguzi wa kimataifa kama vile Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA au Shirika la Ujasusi la Israel, Mosad. Alisema kutokana na uwezo wao mkubwa kuchunguza, watapata suluhu kirahisi zaidi kuhusu tukio hilo.Aliitaka serikali kutambua kuwa kwa kuruhusu uchunguzi wa kimataifa, haimaanishi kuwa nchi haina uwezo wa kuchunguza. Alisema mijadala mingi inayoendelea kwenye mitandao ya kijamii, inadhihirisha kuwapo kwa kiu ya majibu kutokana na mkasa huo.Hivyo, alimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola kufuta katazo la watu kumjadili MO Dewji kwenye mitandao ya kijamii. Pia aliwataka viongozi wa dini, asasi za kijamii, wasomi, wanahabari na jamii, kukemea matukio ya utekaji, kwa kuwa ni mabaya na yakiachwa yataendelea kusababisha balaa zaidi kwenye jamii.
3
Na MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limeanza operesheni ya kuwaondoa wakazi wanaoishi mabondeni ili kuepukana na adha ya mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Hatua hiyo inatokana na kutokea kwa maafa ya vifo yaliyosababishwa na mvua zilizoanza kunyesha tangu mwishoni mwa mwezi uliopita. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro, alisema jana kuwa mvua zilizonyesha juzi zimesababisha maafa baada ya mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mongo la Ndege, Imelda Ngonyani (13), kufariki dunia wakati akivuka Mto Msimbazi eneo la Mongo la Ndege. Alisema mwanafunzi huyo alifariki alipokuwa akijaribu kuvuka Mto Msimbazi kuelekea shuleni akiwa na wanafunzi wenzake watano. “Tumeanza operesheni ya kuwaondoa watu wanaoishi katika maeneo hatarishi, hasa katika Bonde la Mto Msimbazi, hatuwezi kuacha watu wafe wakati tuna dhamana ya kuwalinda. Wananchi wakubali kuhama kwa hiari la sivyo tutawaondoa kwa nguvu,” alisema Sirro. Katika hatua nyingine, jeshi hilo limefanikiwa kuwaua majambazi wawili ambao walikuwa wanajiandaa kufanya uhalifu katika eneo la Kigamboni. Kwa mujibu wa Sirro, Jumapili iliyopita saa 3:35 usiku walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu kuwapo kwa watu watatu waliopanga kufanya uhalifu katika eneo la Zimbwini Vijibweni ndipo waliweka mtego na kufanikiwa kuwakamata. Alisema baada ya majibizano ya risasi, majambazi wawili waliuawa na polisi walifanikiwa kukamata bastola moja aina ya bereta ikiwa na risasi sita. Katika hatua nyingine, Kamanda Sirro alisema kuwa jeshi hilo limefanikiwa kukamata watuhumiwa 110 wa makosa mbalimbali ya uhalifu yakiwamo kupatikana na dawa za kulevya, bangi, unyang’anyi wa kutumia silaha, utapeli na kuuza pombe haramu ya gongo. Kamada Sirro alisema walikamata kete 102 za dawa za kulevya, puli 95, misokoto ya bangi 106 na lita 10 za pombe haramu ya gongo. Kuhusu msako wa pombe zinazofungashwa katika mifuko ya plastiki maarufu viroba,  alisema Machi 10, mwaka huu walimkamata mmiliki wa duka la kuuza vileo vya jumla na rejareja katika eneo la Banana akiwa na katoni 175 za viroba. Alisema mfanyabiashara huyo alikutwa na katoni 155 dukani kwake na katoni 20 zilikutwa nyumbani kwake baada ya upekuzi. Kamanda Sirro pia amepiga marufuku askari wa jeshi hilo kumwaga vyakula katika kumbi za burudani badala yake kama mtu amevunja sheria achukuliwe kwa utaratibu pamoja na vyakula vyake. “Kila uhuru una mipaka yake, kuna klabu zina leseni na nyingine huwa zinaenda mpaka saa 11 alfajiri na huwa kuna biashara za vyakula zinaendelea. Askari wasiwazuie kwa sababu wako ndani ya utaratibu,” alisema.
3
SERIKALI imewataka wananchi walio- athirika na milipuko ya mabomu ya Mbagala mwaka 2009 na Gongo- lamboto mwaka 2011 jijini Dar es Salaam, kufika kwenye ofisi za wakuu wa wilaya ya Temeke na Ilala kwa uhakiki wa malipo ya fidia. Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa jana na Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Abubakar Kunenge, kwenye gazeti la Serikali la Daily News, waathirika hao wanatakiwa kwenda na vielelezo vya kuthibitisha uhalali wa madai yao. Kunenge aliyataja makundi ya wananchi wanaolengwa katika uhakiki huo kuwa ni wale ambao hawaku- hakikiwa na kamati teule ya serikali katika awamu tano za uhakiki zilizopita. Wengine ni waliohakikiwa na kukidhi vigezo vya kulipwa fidia kama ilivyopendekezwa na kamati teule lakini bado hawajalipwa fidia hiyo, pamoja na ambao taarifa zao hazikukamilika kwa ajili ya tathimini ya fidia.Alisema wananchi hao wanatakiwa kuwa na vielelezo vinavyotakiwa wanapokwenda kukutana na kamati ya uhakiki. Kwa mujibu wa tangazo hilo, waathirika kutoka wilaya ya Temeke wanatakiwa kukutana na kamati hiyo katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Temeke na kamati ilianza kazi hiyo ya uhakiki tangu jana na itakamilisha Septemba 30, mwaka huu. Kwa upande wa wananchi wa Ilala, wanatakiwa kuku- tana na kamati hiyo Oktoba Mosi na Oktoba 2 katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ilala. Kunenge aliwata wananchi wenye madai kuwasilisha vielelezo visivyo na shaka pamoja na barua za utambulisho kutoka ofisi za watendaji kata, lakini pia wakumbuke kuwa orodha ya waathirika inapatikana katika ofisi za watendaji wa kata. Hata hivyo, serikali imeonya kuwa, mwananchi atakayewasilisha maelezo au nyaraka zitakazothibitika kuwa za kughushi au za udanganyifu kwenye ngazi ya kata au mbele ya kamati kwa lengo la kulipwa fidia asiyostahili au kuiibia serikali, atachukuliwa hatua za kisheria. Aprili, 2009, mabomu katika Kambi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) eneo la Mbagala yalilipuka kwa mfululizo na kusababisha vifo na majeruhi kwa watu kadhaa pamoja na kuharibu baadhi ya nyumba na mali nyingine. Tukio kama hilo lilitokea tena Februari 2011, ambapo mabomu katika Kambi ya JWTZ Gongolamboto yalilipuka na kusababisha vifo na majeruhi kwa watu kadhaa na kuharibu baadhi ya nyumba na mali nyingine. Mkazi wa Gongolamboto, Abeli Mwaikasu, akizungumzia kuhusu wito huo wa serikali jana, alisema unadhi- hirisha nia njema ya serikali ya kuwatumikia wananchi wanyonge ambao waliathiriwa kwa kiwango kikubwa na matukio hayo.
3
    Na OMARI MLEKWA-HAI SERIKALI wilayani Hai  Mkoa wa Kilimanjaro, imeondoa miundombinu ya uzalishaji katika shamba la Kilimanjaro Veggies linalomikiwa na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe  (Chadema). Miundombinu hiyo iliondolewa jana kwa vile shamba hilo liko ndani ya chanzo cha maji ya Mto Weruweru. Pamoja na kuondoa miundombinu hiyo, Serikali imemtaka Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema   alipe Sh milioni 18 kutokana na uharibifu wa mazingira aliofanya kwenye chanzo hizo. Pia, Mbowe ametakiwa kulipa gharama zote zilizotumika kuondoa miundombinu kwenye shamba hilo. Uamuzi huo umefikiwa  baada ya Mbowe kudaiwa kukaidi amri aliyopewa na Serikali ya kusimamisha kilimo cha mboga mboga katika eneo hilo lenye ukubwa wa ekari mbili, lililopo Kijiji cha Nshara. Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gellasius Byakanwa, alisema wameamua kuondoa miundombinu yote iliyokuwa ikitumika kwenye shamba hilo baada ya Mbowe kupewa miezi minne kuiondoa kwa hiari na kushindwa kutekeleza agizo hilo. “Januari 23 mwaka huu, Freeman Mbowe, alifika ofisini kwangu akiwa na wanasheria wake kutokana agizo nililotoa kwa ajili ya kusimamisha shughuli za  binadamu katika shamba lake hilo. “Tulikubaliana atatumia miezi minne kuondoa mazao yaliyokuwa kwenye shamba hilo na miezi minne hiyo imeishia Mei 23, mwaka huu. “Huyo ni kiongozi na ni kioo cha jamii, haipendezi kufanya vitu kama hivi kwa sababu pia wajibu wa wananchi ni kutunza vyanzo vya maji,” alisema Byakanwa. Mkaguzi wa Mazingira wa Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira (NEMC), Kanda ya Kaskazini, Novatus Mushi, alisema uamuzi waliochukua unatokana na Mbowe kushindwa kufuata sheria ya mazingira ya mwaka 2,004. Alisema kifungu 81 kinamtaka kila mtu anayeanza mradi wa kilimo kufanya tathinimi ya uharibifu wa mazingira lakini mmiliki huyo hakufanya na wala hakushirikisha mamlaka husika. “Mmiliki huyo alikiuka sheria ya mazingira kifungu cha 51 kinachokata mtu yeyote yule kutokufanya shughuli za mazingira ndani ya eneo  la mita 60 kando ya chanzo cha maji lakini mtu huyo amefanya hivyo alivyotakiwa kuondoa amekaidi. “Pia kifungu namba 200 b cha sheria ya mazingira kinataka mtu yeyote yule anayepewa mazingizo na mamlaka  za nchi ikiwamo kukataza shughuli za  binadamu ndani ya maeneo yanayolindwa kisheria afanye hivyo kwa mujibu wa muda aliyopewa na mamlaka husika. “Huyo bwana alipewa miezi minne aondoke kwa hiari yake na ofisi ya mkuu wa wilaya hakufanya hivyo mpaka leo hii tunapochukua hatua  bado shughuli za uzalishaji zilikuwa zikiendelea katika shamba hili. “Kwakifupi ni kudharau mamlaka sababu ni mamlaka iliyopo kisheria na imempa agizo lilipo kisheria “Pia sisi tulimwandikia barua Juni 6 mwaka huu ikimkumbusha asimamishe shughuli za binadamu katika eneo hilo, ambayo iliambatana naadhabu ya kumtaka kulipa Sh milioni 18 kutokana uharibifu wa mazingira katika chanzo hicho maji cha mto Weruweru,” alisema.
3
Akizungumza jana kuhusu taarifa ya soko katika mauzo yaliyofanyika wiki iliyopita, Meneja Miradi na Biashara wa DSE, Patrick Mususa, alisema idadi ya mtaji wa soko imeshuka kutoka Sh trilioni 21.0 hadi Sh trilioni 20.2.“Kiasi hicho kinaonesha kuwa bei za hisa za makampuni zimepungua kwa asilimia 3.9,” alisema Mususa wakati akitoa taarifa ya DSE kwa mnada uliofanyika wiki iliyopita.Aliongeza kuwa idadi ya mtaji wa makampuni ya ndani imeshuka pia kutoka Sh trilioni 9.7 hadi Sh trilioni 9.4.Katika mnada huo, Benki ya CRDB ilichangia zaidi ya asilimia 75 ya idadi ya mauzo yote ya wiki iliyopita, ingawa bei ya hisa zake ilishuka kwa asilimia 1.23.Alisema idadi ya mauzo ya hisa, imeongezeka wiki iliyopita yameongezeka kwa asilimia 50 hadi kufikia Sh bilioni 6.7 kutoka bilioni 4.4.Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa, imepanda zaidi ya mara nne hadi Sh milioni 12.8 kutoka milioni 3.6.Alitaja kampuni tatu zinazoongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa kuwa ni Benki ya CRDB kwa asilimia 98.45, Kampuni ya Bia (TBL) asilimia 0.75 na Kampuni ya Saruji Tanga (TCCL) kwa asilimia 0.34.“Hii inaonesha kuwa CRDB ilichangia zaidi ya asilimia 75 ya idadi ya mauzo ya wiki hii ingawa bei yake ilishuka kwa asilimia 1.23,” alisema Mususa.Kwa upande wa viashiria, Mususa alisema kiashiria cha sekta ya viwanda kimeshuka kwa pointi 4.33, kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa kwenye kaunti za TCCL kwa asilimia 0.75 na Kampuni ya Saruji ya Twiga (TPCC) kwa asilimia 0.67.Alisema kiashiria cha sekta ya huduma za kibenki na za kifedha, kimeshuka kwa pointi 113.23, kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa kwenye kaunta za Benki ya NMB kwa asilimia 6.12 na CRDB kwa asilimia 1.23.“Kiashiria cha sekta ya huduma za kibiashara kimeshuka kwa pointi 16.75 kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa kwenye kaunta ya Swissport kwa asilimia 0.55,” alisema Mususa.
5
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amewaagiza viongozi wa Mkoa wa Mtwara kukaa chini na kutafakari namna wanavyosimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo hususani ujenzi wa vituo vya afya mkoani humo.Alitoa agizo hilo mjini hapa jana baada ya kutembelea ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mtimbwilimbwi kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba mkoani hapa kwa lengo la kujionea namna ambavyo ujenzi huo unaendelea.Alisema, miradi mingi ya afya inayotekelezwa mkoani humo haiendi vizuri ikilinganishwa na miradi inayotekelezwa katika mikoa mingine nchini.“Tatizo ninaloliona hapa, ni usimamizi wa viongozi na hapa sijafika Masasi inawezekana tatizo likawa ni hili hili. Nimekwenda pale Nanguruwe hali ni mbaya zaidi, nilitarajia kwamba nikifika Mtwara majengo yote yawe yamekamilika, lakini kasi hairidhishi kabisa,” alisema.Waziri Jafo pia alitembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya inayotarajiwa kujengwa eneo la Nanguruwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ambapo alikuta ujenzi wake haujaanza na kuagiza kuwa hadi kufikia Juni 10, mwaka huu, uwe umeshaanza.Pia alitembelea ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mkunwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ambako tayari ujenzi wake umeshaanza kutekelezwa huku zaidi ya Sh milioni 200 zikiwa tayari zimeshatumika.“Naagiza, hadi kufikia tarehe 30, mwezi huu, majengo yote yawe tayari yamekamilika na napenda niseme wazi kabisa kuwa Mtwara hamna rekodi nzuri katika utekelezaji wa miradi hii. Naagiza hadi tarehe 30, mwezi huu miradi hii iwe imekamilika.”Kwa upande wake, mkazi wa Nanyamba, Abdurazaki Kasembe alisema kusuasua kwa Kituo cha Afya cha Nanyamba kunatokana na viongozi wa mkoa kuwa chanzo cha kukwamisha miradi hiyo kwani wamekuwa na mvutano wa wenyewe kwa wenyewe.
3
WATU wengi wanahofiwa kufa maji kutokana na kuzama kwa Kivuko cha Mv Nyerere kilichokuwa kikifanya safari yake kutoka Kisiwa cha Bugolora kwenda Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza katika Ziwa Victoria jana.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shana alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo mchana na kusema hatua mbalimbali zimechukuliwa ili kujaribu kuokoa watu walio hai na kuopoa miili ya watu waliopoteza maisha.Hadi tunakwenda mitamboni jioni miili ya watu watano ilikuwa imeopolewa majini wakiwa tayari wamepoteza maisha huku wengine 32 wakiookolewa wakiwa hai, wengi wao wakiwa katika hali mbaya na kukimbizwa katika Kituo cha Afya cha Ukara kwa msaada wa matibabu.Kamanda huyo wa Polisi aliwaambia waandishi wa habari kuwa kivuko hicho kilipoteza uwezo wake wa kawaida majini kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha mizigo na abiria.Alisema Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela baada ya kutokea kwa tukio hilo, aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kwenda kwenye eneo la tukio umbali wa saa tatu kutoka Mwanza mjini.Ingawa Kamanda huyo wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza hakuweza kutaja idadi ya watu waliokuwa ndani ya kivuko hicho wakati kinazama, mmoja wa maofisa wa serikali alisema kulikuwa na zaidi ya watu 100 waliokuwa wakitoka kwenye mnada.Wakala wa Taifa wa Ufundi na Umeme (Temesa) ambaye ndiye mwendeshaji wa vivuko vyote nchini, kupitia taarifa yake kwa umma jana, ulithibitisha kutokea kwa tukio hilo la kusikitisha.Kupitia taarifa hiyo, Temesa iliwataka wananchi kuwa watulivu hadi taarifa rasmi kuhusiana na tukio hilo zitakapotolewa baadaye. Wasemavyo mashuhuda Mashuhuda walisema kivuko hicho kilikuwa kinatokea Bugolora kwenda Ukara kati ya saa 6 na saa 7.30 mchana na kilizama dakika kama tano kabla ya kufika kwenye ghati ya Ukara.Walisema ghafla waliona kivuko hicho kikianza kutitia kwenye maji kwa nyuma kulikokuwa na mizigo na kuwezesha abiria waliokuwa mbele kurukia majini na kuogelea na mitumbwi iliyokuwa hapo kufanya kazi ya kuwaokoa abiria waliorukia majini.Inasemekana abiria wengi waliokuwa ndani ya Mv Nyerere hawakuweza kutoka na kuwa wamezama, huku wakidai kivuko hicho kina uwezo wa kubeba abiria 150.Walisema Meli ya Mv Clarias ilikuwa imeshaondoka kama dakika 10 kabla ya tukio lakini ikaamriwa kurudi na kushusha abiria na kuelekea Ukara kushiriki zoezi la uokoaji.Walisema Mv Nyehunge pia ilishusha abiria na mizigo na kuelekea Ukara kushiriki zoezi hilo. Kumbukumbu za ajali za majini Tukio la kuzama kwa tukio hilo limeibua hisia za kumbukumbu za ajali mbaya iliyowahi kutokea katika ziwa hilo pale meli ya Mv Bukoba ilipozama na kuua watu zaidi ya 1,000.Meli hiyo ilipatwa na zahama hiyo ikiwa safarini kuelekea Mwanza Mei 21, mwaka 1996, wakati ikiwa imebakiza mwendo mfupi kufika Bandari ya Mwanza. Mamlaka zilieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ilikuwa ni meli hiyo kubeba kiwango kikubwa cha abiria na mizigo zaidi ya uwezo wake.Tukio jingine baya la kuzama kwa meli, lilitokea Septemba 10, 2011, ambapo karibu abiria 200 walipoteza maisha baada ya meli ya Mv Spice Islander, ilipozama ikitoka Unguja kwenda Pemba katika mkondo wa Nungwi.
3
NA EVANS MAGEGE – DAR ES SALAAM BENKI ya NBC imetangaza kuvipiga mnada shule na vyuo vya Eckernforde vya mkoani Tanga. Kwa mujibu wa tangazo la benki hiyo lililotolewa katikati ya wiki hii na Kampuni ya udalali ya Bani Investment Limited, Debt Collectors/Auctioneers na kuchapishwa katika magazeti mawili ya kila siku (si MTANZANIA Jumapili), limetanabaisha kuwa mnada wa chuo hicho pamoja na shule zake utafanywa Machi 11. Akithibitisha taarifa hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Bani, Lita Colyvas, alisema taratibu za kutekeleza mnada wa vyuo vya Eckernforde umefuatwa kisheria. “Ni kweli sisi ndio tumetangaza mnada huo kwa niaba ya Benki ya NBC, tumetoa tangazo siku 14 kabla ya mnada na siku tatu kabla ya mnada tutatangaza tena, ikiwapo kupitisha gari la matangazo mtaani,” alisema Colyvas. Alivitaja vyuo hivyo kuwa ni kile kilichojengwa kwenye kiwanja namba 53/2 na kiwanja namba 54/2, CT namba 2532, LO namba 62988, kitalu 111 chenye ukubwa wa mita za mraba 921 ambacho kipo eneo la Central Tanga. Chuo kingine ni cha ualimu pamoja na sekondari ambacho kina ukubwa wa ekari 3,426 kwenye kiwanja namba 12, CT namba 18517, LO namba 170760 katika eneo la Kange Tanga. Alisema kuwa vyuo hivyo vinatambulika kwa jina la Eckernforde Education Company Limited.
3
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo ameagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha zinafungua akaunti maalumu kwa ajili ya asilimia 10 ya fedha za mapato ya ndani, kwa ajili ya mikopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.Aidha, aliahidi kuangalia namna wizara yake itakavyotenga fedha kwa ajili ya wataalamu wa maendeleo ya jamii, zitakazotumika kwa ajili ya ufuatiliaji na tathimini ya fedha zinazotolewa kwenye vikundi.Jafo aliyasema hayo wakati wa kufunga kongamano la wataalamu wa maendeleo ya jamii uliofanyika jijini hapa. “Niliwahi kutoa agizo la kutaka halmashauri kufungua akaunti maalumu kwa ajili ya fedha za mikopo ya makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ingawa sijajua utekelezaji wake. Lakini sasa naagiza kwa mara ya mwisho ikifika Novemba 30 mwaka huu, halmashauri zote zihakikishe zimefungua akaunti hiyo.Akizungumzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Jafo aliwataka maofisa maendeleo ya jamii kwenda kuhamasisha watu wachukue fomu za kuwania nafasi mbalimbali na pia kushiriki kupiga kura. Jafo alisema halmashauri tano zitakazofanya vizuri katika uhamasishaji huo zitapewa zawadi kwa maofisa maendeleo watakaokuwa katika maeneo hayo kwa ajili ya kusimamia uchaguzi.Pia, Jafo aliahidi kuhakikisha kunakuwa na fungu kwa ajili ya kwenda kusimamia kazi mbalimbali za maendeleo ya jamii katika maeneo tofauti na upatikanaji wa vifaa, yakiwemo magari.Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk John Jingu, alisema anaamini baada ya kongamano hilo maendeleo ya jamii wataleta maendeleo katika maeneo yao na kuamsha ari ya wananchi kushiriki miradi ya maendeleo inayoletwa na serikali.Kwa upande wa Rais wa Chama cha Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii (CODEPATA), Sunday Wambura, alisema chama hicho kitatekeleza maagizo yaliyotolewa na waziri wa afya, lengo likiwa kuhamasisha maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini.
3
NA MASYENENE DAMIAN MAKAMU wa Rais, Samia Hassan Suluhu ameahidi kuchangia mifuko 200 ya saruji na mabati 100 kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika shule ya sekondari ya Askofu Anthony Mayalla wilayani Kwimba. Aliahidi mchango huo wakati akiweka jiwe la msingi katika   mabweni ya wasichana katika shule hiyo  kuunga mkono jitihada zinazoonyeshwa na shule hiyo za kuwaokoa watoto wasichana dhidi ya vishawishi mbalimbali vinavyokatisha masomo yao. “Naahidi kuchangia mifuko ya saruji 200 ambako 100 itatoka ofisi yangu na 100 itatoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa (Mwanza) na mabati 100 lakini pia Mbunge (Richard Ndassa) na wewe uchangie mabati 100,” alisema. Shule ya Askofu Mayalla inahudumia wasichana ambao walikumbwa na matatizo ya mimba za utotoni na kukosa karo. Akizungumzia changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo, Katibu wa Askofu wa Jimbo Kuu la Mwanza, Moses Mapela, alisema  kubwa   ni upungufu wa vyumba vya madarasa, mabweni, maktaba, ukosefu wa gari la shule, uzio, kompyuta na udhibiti wa nidhamu shuleni hapo. “Shule yetu ilianzishwa mwaka 2010 ikiwa na wanafunzi 68 lakini hivi sasa tunao wanafunzi 456 walimu 18 na wafanyakazi 15 na tuna mpango wa kuanzisha kidato cha tano na sita. “Lengo kuu la shule yetu ni kuwapatia fursa ya kurudi shule na kuendelea na masomo watoto wa kike waliokosa fursa hizo kwa kupewa mimba ama kukosa karo,” alisema. Ujenzi wa bweni hilo unatarajiwa kukamilika Januari mwakani kama wadau watajitokeza kusaidia na linatarajiwa kugharimu Sh milioni 157 na tayari limeshatumia Sh milioni 27 huku likitegemewa kuchukua wanafunzi wa kike 120 kwa wakati mmoja. Shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2010 na aliyekuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Mwanza, Marehemu Anthony Mayalla.  Kutoka Sengerema,  ANNA RUHASHA anaripoti kuwa   Samia alifungua bweni la wasichana la Chuo cha Utabibu wilayani Sengerema   lenye thamani ya Sh milioni 655 lililojengwa na Kanisa Katoliki. Samia aliiomba taasisi hiyo kujenga kituo cha afya mkoani Geita  kupunguza mzingo  wa wingi wa wagojwa wanaotafuta huduma katika hospitali ya mkoa wa geita na hospitali jirani ya teule ya Wilaya ya Sengerema DDH. Mkuu wa chuo hicho Dk. Dickson Materu  alisema ujenzi wa bweni hilo ni katika mpango   wa    jimbo  wa mwaka 2011/2016 ambako  mradi huo  utaongeza idadi ya watalaamu  wa afya ya msingi hapa nchini na kuboresha  utoaji wa huduma ya tiba  katika taifa. Askofu wa Jimbo la Geita, Mhashamu Flavian Mtinda Kassala aliiomba Serikali kuangalia namna ya kuzipatia msamaha wa kodi ili kuhakikisha wanaondokana na changamoto wanazokabiliana nazo katika kuendesha taasisi hiyo ambayo inafanya kazi na serikali.
3
THARAKA NITHI, KENYA MGOMBEA urais kupitia muungano wa upinzani wa NASA, Raila Odinga atahudumu urais kwa muhula mmoja iwapo atashinda, Kiongozi wa Chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka amesisitiza. Kalonzo ambaye ni mgombea mwenza wa Raila, amewahakikishia wafuasi wake kauntini hapa juzi kuwa hakuna mgombea mwingine wa upinzani atakayepingana naye katika uchaguzi wa mwaka 2022. Akizungumza kwa lugha ya Kikamba, makamu huyo wa zamani wa rais alisema. “Bila kuficha chochote kwenu, Raila Odinga atashikilia kiti cha urais kwa muhula mmoja wa miaka mitano kama tulivyokubaliana kimaandishi, si kama makubaliano ya nyuma yasiyo rasmi. “Sasa ni wazi tumekubaliana Raila atasaidia kuihamisha Kenya katika kiwango kingine cha mafanikio na mwaka 2022 atakuwa Kalonzo Musyoka mwenye jukumu hilo. Hakuna lingine,” alisisitiza. Kiongozi huyo wa Wiper alisema upinzani unaelekea kupata ushindi dhidi ya Jubilee na alikituhumu chama tawala kwa njama za kuleta wasiwasi wa kisiasa katika ngome za NASA. “Tunawahimiza wafuasi wetu kuwa macho na kulinda katika vituo vya kura kwa sababu tuna taarifa Jubilee imekula njama za kuwatisha wapiga kura kutoka jamii fulani waliopo katika miji mikubwa,” Kalonzo alisema na kuongeza kuwa kila Mkenya ana haki ya kupiga kura.
2
NA MWALI IBRAHIM NA JULIET MORI (TUDARCO) MWAMUZI Israel Nkongo anayetambulika na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), anatarajiwa kuamua mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Azam na Yanga, utakaochezwa Jumamosi hii, Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Nkongo ana historia kubwa na mechi hiyo kwani aliwahi kuchezesha mechi ya ligi ya miamba hiyo Machi 2012, lakini mchezo huo ulioishuhudia Azam ikitoka kifua mbele kwa kushinda 3-1, ulimalizika kwa Nkongo kupata mkong’oto kutoka kwa wachezaji wa Yanga, baada ya kuwaonyesha kadi nyekundu wachezaji wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Haruna Niyonzima, hali iliyoamsha vurugu kubwa kutoka kwa mashabiki na wachezaji hao. Hali hiyo ilipelekea Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kutoa adhabu kwa wachezaji watano wa Yanga na timu kupigwa faini ya Sh 500,000 kutokana na washabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi hiyo Machi 10, 2012, pia klabu hiyo ilipigwa faini ya Sh 500,000 kwa mujibu wa Kanuni ya 25(d) baada ya kuoneshwa kadi kuanzia tano kwenye mechi hiyo. Kutokana na vurugu hizo, Cannavaro alifungiwa mechi sita za Ligi Kuu na kupigwa faini ya Sh 500,000 baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwa kosa la kumshambulia mwamuzi, Israel Nkongo kwenye mechi hiyo, huku wachezaji wengine wa Yanga walioadhibiwa kutokana na mechi hiyo ni Nurdin Bakari alifungiwa mechi tatu na faini ya Sh 500,000, Omega Seme alifungiwa mechi tatu na faini ya Sh 500,000, Jerryson Tegete aliyefungiwa miezi sita na faini ya Sh 500,000, wakati Stephano Mwasika, alifungiwa mwaka mmoja na faini ya Sh milioni moja. Lakini Kamati hiyo ilimpongeza aliyekuwa nahodha wa Yanga, Shadrack Nsajigwa na aliyekuwa mshambuliaji wa timu hiyo, Hamis Kiiza, kwa kuwa mstari wa mbele kuzuia wenzao kumshambulia mwamuzi, ilimpongeza pia aliyekuwa Kocha Mkuu, Kostadin Papic kwa kukemea vurugu zilizofanywa na wachezaji wake. Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto, alisema mwamuzi huyo atasaidiwa na Samwel  Mpenzu (Arusha), Josephat  Bulali (Tanga), mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah (Dar es Salaam) na kamisaa wa mchezo huo ni Deogratius Rwechungura kutoka mkoani Mara Alitaja viingilio vya mchezo huo kuwa ni Sh 7,000 kwa viti vya rangi ya kijani, bluu na rangi ya chungwa, VIP B na  C Sh 20,000 na VIP A Sh 30,000 ambapo tiketi zitaanza kuuzwa siku ya mchezo maeneo ya uwanja huo. Wakati huo huo, Ofisa habari wa klabu ya Azam, Jaffar Iddi, amesema wapo katika maandalizi ya mwisho ya mchezo huo lakini watawakosa wachezaji wao Michael Balou ambaye ni majeruhi na Allan Wanga ambaye yuko kwao msibani. “Tumejiandaa kikamilifu na tunaendelea kujiandaa lakini tutawakosa wachezaji hao wawili kutokana na matatizo tofauti, lakini wachezaji wengine wako fiti na tuna imani tutashinda,” alisema.
4
KATIBU Mkuu wa zamani wa Shirikisho la Soka la Kenya (KFF), Hussein Swaleh ni miongoni mwa watu 157 waliokufa katika ajali ya ndege ya Ethiopia iliyoanguka juzi asubuhi ikitoka Addis Ababa kwenda Nairobi.Swaleh alikuwa akirejea kutoka katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Ismail ya Misri na TP Mazembe ya Congo DR zilizocheza mjini Cairo, Misri, Ijumaa iliyopita, Swaleh akiwa kamishna wa mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1.Katibu Mkuu wa Baraza la vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) Nicholaus Musonye alisema jana, Baraza lake limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mdau huyo na kuiombea faraja familia yake pamoja na wakenya kwa ujumla.Kwa mujibu wa taarifa kutoka shirika hilo la ndege, watu wote 157 waliokuwa ndani ya ndege hiyo walikufa. Taarifa hiyo iliongeza kuwa, kulikuwa na watu kutoka mataifa 33 katika ndege hiyo iliyoanguka dakika sita baada ya kuruka kutoka kwenye Kiwanja cha Addis Ababa, Ethiopia. Ndege hiyo ilianguka saa 2:44 kwa saa za Ethiopia, ikiwa ni dakika sita baada ya ndege hiyo kuruka katika mji mkuu huo wa Ethiopia.
4
MFUMUKO wa Bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia Septemba, mwaka huu, umepungua hadi asilimia 3.4 kutoka asilimia 3.6 kwa mwaka ulioishia Agosti, mwaka huu.Kupungua huko kunatokana na bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Septemba, mwaka huu kupungua ikilinganishwa na kasi iliyokuwapo kwa mwaka ulioishia Agosti mwaka huu.Hayo yamesemwa jijini hapa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa za Jamii, Ruth Davison, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya mfumko wa bei kwa ajili ya matumizi ya serikali na wadau wa takwimu.Alisema kupungua kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Septemba, mwaka huu, kumechangiwa hasa na kupungua kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Septemba, mwaka jana.“Baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizopungua bei ni mafuta ya taa kwa asilimia 1.0, petroli kwa asilimia 3.3, majiko ya gesi kwa asilimia 1.5, dawa ya kuulia wadudu nyumbani kwa asilimia 2.2 na mafuta ya nywele kwa asilimia 1.3,” alisema.Hata hivyo, alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwaka ulioishia Septemba, mwaka huu, umeongezeka hadi asilimia 4.0 kutoka asilimia 3.7 kwa mwaka ulioishia Agosti mwaka huu.
5
Na ASHA  BANI-DAR ES SALAAM NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, amesema kuanzishwa kwa mradi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), kutasaidia kukuza uchumi wa nchi. Ulega ambaye pia ni Mbunge wa Mkuranga, amesema mradi huo ambao ulianzishwa na Kampuni ya Raddy Fibre Solution (LTD) unatarajiwa kutandaza mkongo wa Taifa katika wilaya 185 ikiwemo Mkuranga Akizungumza na ujumbe wa kampuni hiyo mwishoni mwa wiki wilayani Mkuranga, alisema kukamilika kwa mfumo huo kutaisadia wafanyabiashara wenye viwanda kujua hali ya masoko ya ndani na nje haraka. “Hivi sasa serikali ipo katika harakati za kukuza uchumi kupitia viwanda na kama mnavyofahamu Mkuranga ni eneo maalumu la kimkakati la viwanda ambalo linatakiwa kuwa na mawasiliano ya uhakika. “Ufungwaji wa mfumo huu Wilaya ya Mkuranga utaiunganisha wilaya yetu, wamiliki wa viwanda pamoja na wana Mkuranga,” alisema Ulega Hivi karibuni  Mkurugenzi wa halmashauri hiyo,Mhandisi Mshamu Munde akiwa katika mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (ALAT) alisema hatua za awali za mpango huo zitakuwa na manufaa kiuchumi. Alisema mfumo huo ambao unafahamika kama e-LGA unafanana na mfumo wa Serikali Mtandao (e-Gorvement) hivyo utasaidia kufanya kazi za mawasiliano kwa urahisi zaidi. “Imefika wakati sasa kwa wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kutumia mfumo huo kwa kuwa utakuwa na manufaa katika kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla hasa kwa ngazi za halmashauri. “Pia utakuwa na manufaa zaidi hasa kusaidia kurahisisha mpango wa malipo, kuingiza taarifa za afya za wilaya na hata shughuli za kiuchumi kama vile kilimo na mifugo na mifumo mingineyo “Utasaidia kuunganisha masoko kwa wafanyabiashara, wakulima wa nyanya Iringa kuweza kufanya biashara na wakulima wa mpunga Mbeya na Korosho Mkuranga kwa kuwasiliana kupitia mkongo wa mawasiliano.
3
MOSCOW, URUSI SERIKALI ya Urusi imetoa kaul dhidi ya matamshi ya Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki aliyesema kuwa nchi hiyo inaingilia vita nchini Libya na kueleza kuwa, matamshi hayo hayana ukweli wowote. Msemaji wa Ikulu ya Kremlin, Dmitry Peskov, alisema jana kuwa, matamshi ya Rais wa Uturuki kwamba Urusi imekuwa na ushiriki wa kiwango cha juu kabisa katika vita vya Libya si ya kweli. Ofisa huyo wa Ikulu ya Rais nchini Urusi alieleza wazi kwamba, Rais Vladimir Putin hajatoa amri ya kutumwa vikosi vya kijeshi vya nchi hiyo huko nchini Libya. Hayo yanajiri katika hali ambayo, Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya imeendelea kukosoa uingiliaji wa nchi za kigeni na misaada yao kwa wapigani wa jenerali muasi, Khalifa Haftar. Mgogoro wa Libya ulichukua sura mpya Aprili mwaka jana baada ya kundi linalojiita jeshi la Taifa la Libya linaloongozwa na jenerali muasi, Khalifa Haftar kuanzisha mashambulizi makali kwa ajili ya kuuteka mji mkuu wa Libya Tripoli unaodhibitiwa na Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya. Nchi za kiarabu, Saudi Arabia, Misri na baadhi ya madola ya Ulaya yamekuwa yakimuunga mkono jenerali Khalifa Haftar na hata kumpatia misaada ya hali na mali.  Uturuki nayo imekuwa ikiipatia misaada ya kijeshi Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya inayotambuliwa na jamii ya kimataifa licha ya vikwazo vya silaha vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa dhidi ya nchi hiyo.
2
Na ASHA BANI, WANACHAMA wa Chama cha Wananchi (CUF) wanaomuunga mkono Katibu Mkuu wa Chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, wametakiwa kutomjadili  Mwenyekiti wa Chama hicho anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Profesa Ibrahimu Lipumba. Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa chama hicho, Salim Bimani, imewataka viongozi wa CUF, wanachama na wapenda mabadiliko nchini, kumpuuza Lipumba kwa kile walichosema anatumiwa na baadhi ya viongozi. Katika maelezo hayo, Bimani alisema wamepokea taarifa za kusajiliwa kwa bodi feki ya Lipumba na baadaye Juni 24, mwaka huu, Lipumba alikaririwa akisema anataka kuwahoji Maalim Seif, Nassor Mazrui (Naibu Katibu Mkuu-Zanzibar) na viongozi wengine wa chama hicho. “Tunapenda kuwajulisha wanachama na viongozi wetu wote wa chama, wabunge, madiwani, viongozi wa halmashauri zote, wenyeviti wa mitaa, vijiji, vitongoji, wapenda mabadiliko na Watanzania kwa ujumla, kuwa CUF kupitia vikao halali vya chama, vilishafanya uamuzi juu ya Lipumba na wenzake, kwamba huyo si mwenyekiti tena. “Anachokifanya Lipumba ni mwendelezo wa kuhakikisha dhamira yake ya kutaka kuivuruga CUF inatimia ili kuzuia haki na uamuzi wa Wazanzibari walioufanya Oktoba 25, mwaka 2015, haipatikani. “Kwa ujumla, CUF na viongozi wake wamejipanga vema kukabiliana na usaliti huo na hakuna kiongozi au mwanachama yeyote atakayekwenda kuhojiwa na Lipumba.
3
CHUO Kikuu Huria nchini (OUT) kimeshika nafasi ya 13 kati ya vyuo vikuu huria 102 kwa ubora duniani na kwa Afrika kimeshika nafasi ya pili. Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Elifas Bisanda alisema hayo alipokuwa akizungumza na HabariLeo chuoni hapo juzi.Profesa Bisanda alisema Februari, mwaka huu ilitolewa taarifa ya ubora wa vyuo vikuu huria duniani ambapo vipo vyuo vikuu huria 102 kati ya hivyo, OUT imeshika nafasi hiyo ya 13 kwa ubora. Aliongeza kuwa katika Afrika vyuo vikuu huria vipo tisa, chuo hicho nchini kimeshika nafasi ya pili kwa ubora na Chuo Kikuu Huria Afrika Kusini ndicho kilichoshika nafasi ya kwanza. Kwa mujibu wa Profesa Bisanda, katika vyuo vyote 49 vilivyopo nchini, OUT ni namba sita kwa ubora.Kwa upande mwingine alielezea changamoto iliyopo katika chuo hicho kuwa ni Jumuiya ya Watanzania kutoelewa vizuri mfumo wa elimu masafa, wakifikiria kuwa ni elimu ya chini na hafifu. Alisema katika chuo hicho wanafunzi wanakuwa na uelewa mkubwa kwa kuwa hawafundishwi darasani lakini wanapewa maeneo yote ya kusoma ili wayapitie waweze kufanya vizuri katika mitihani yao. “Mtihani unatungwa kulingana na mtaala. Na ubora wa elimu inayotolewa chuoni hapa hauwezi kulinganishwa na vyuo vingine kwa kuwa mwanafunzi anasoma katika wigo mpana,” alisema.Alisema hata wanafunzi wanaomaliza Kidato cha Sita hawaelewi ubora wa elimu unaotolewa na chuo hicho, hivyo wamekuwa wakifanya kampeni shuleni kwa ajili ya kuwaelimisha wanafunzi hao kujiunga na OUT. Mwaka jana chuo hicho kilikuwa na wanafunzi 8,000 lakini sasa wamefikia wanafunzi 12,994 na kabla ya kuondolewa kozi ya foundation mara ya kwanza na hatimaye kurudishwa chuo hicho kilikuwa na wanafunzi 16,000.
3
RAIS John Magufuli amekutana na ujumbe wa Urusi ulioongozwa na Mjumbe Maalum wa Rais wa Urusi masuala ya Afrika, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mikhail Bogdanov, Ikulu, Dar es Salaam.Taarifa iliyotolewa na Ikulu, Dar es Salaam jana ilisema Rais Magufuli amemshukuru Rais wa Urusi, Vladimir Putin kwa ushirikiano na uhusiano mzuri kati ya Tanzania na nchi hiyo na amemhakikishia serikali anayoiongoza inatambua umuhimu wa uhusiano huo na itauendeleza na kuukuza zaidi hususani katika biashara, uwekezaji, utalii na utoaji wa huduma za kijamii kama vile afya, elimu na miundombinu.“Naomba ufikishe ujumbe wangu kwa Rais Putin, Watanzania wanaipenda Urusi na tunamkaribisha kuja kutembelea nchi yetu na wananchi wengine wa Urusi. Tunawakaribisha pia wawekezaji waje wawekeze katika fursa mbalimbali zilizopo hapa kwa manufaa yetu sote,” Rais Magufuli amemweleza Bogdanov.Kwa upande wake, Bogdanov ambaye amewahi kutembelea Tanzania miaka minane iliyopita aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kasi nzuri ya maendeleo iliyoyapata katika kipindi kifupi na alibainisha Urusi imedhamiria kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati yake na Tanzania.Alisema Urusi ina mpango mahususi wa kushirikiana na nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania kuongeza kasi ya maendeleo na hivi karibuni Tanzania na Urusi zitatia saini makubaliano ya kuanzisha tume ya pamoja ya ushirikiano (JPC) katika biashara, uwekezaji na uchumi ili rasilimali na fursa zilizopo katika pande zote zitumike kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizo.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi alisema mazungumzo hayo yamekwenda vizuri na Tanzania inatarajia JPC itakuza uchumi kupitia madini, gesi na utalii hasa wakati huu ambapo Urusi imeitangaza Tanzania nchi yenye vivutio bora vya utalii duniani. Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Meja Jenerali Mstaafu, Simon Mumwi na Balozi wa Urusi nchini, Yuri Popov.
3
Kamusoko na Ngoma ni msimu wao wa kwanza Yanga wakitokea FC Platinums ya Zimbabwe, ambapo Ngoma hadi sasa amecheza mechi 45 na kufunga mabao 24 na Kamusoko amecheza mechi 46 na kufunga mabao tisa katika Ligi Kuu Tanzania Bara.Ngoma mwenye mabao matatu aliyofunga michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika alioneshwa kadi ya pili ya njano katika pambano la marudiano dhidi ya Al Ahly nchini Misri, ambapo kadi yake ya njano ya kwanza aliipata katika pambano la marudiano dhidi ya APR Uwanja wa Taifa Dar es Salaam .Kwa upande wa Kamusoko mwenye mabao mawili, alioneshwa kadi ya njano katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahly pamoja na pambano la kwanza dhidi ya Cercle de Joachim.Hata hivyo, kukosekana kwa wachezaji hao si pigo sana kwani kocha wa Yanga, Hans Pluijm ana hazina ya wachezaji ambao amekuwa akiwaanzisha katika mechi mbalimbali za ligi hiyo hivi karibuni, huku akiwaanzisha benchi Ngoma na Kamusoko.Malimi Busungu ama Paul Nonga mmojawapo anaweza kuchukua nafasi ya Ngoma, huku ile ya Kamusoko akicheza ama Salum Telela, Mbuyu Twite, Said Juma Makapu au Haruna Niyonzima.Yanga imeangukia katika Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF CC), baada ya kutolewa na Al Ahly ya Misri katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2, ililazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam na kufungwa mabao 2-1 Alexandria, Misri.Yanga ilizitoa Cercle de Joachim ya Mauritius kwa mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani kabla ya kuitoa APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2, ikishinda 2-1 Kigali na kutoa sare ya 1-1 Dar es Salaam.Kwa upande wao, Sagrada Esperanca katika Raundi ya Awali waliitoa Ajax Cape Town ya Afrika Kusini kwa mabao 3-2 baada ya kufungwa 2-1 ugenini na kushinda 2-0 nyumbani.Katika Raundi ya kwanza waliitoa LD Maputo ya Msumbiji kwa mabao 2-1, ikishinda 1-0 nyumbani na kutoa sare ya 1-1 ugenini na kwenda hatua ya 16 Bora, ambako waliitoa V. Club Mokanda ya Kongo kwa jumla ya mabao 4-1 wakishinda 2-1 ugenini na 2-0 nyumbani.Vingilio katika mchezo huo utakaochezeshwa na waamuzi kutoka Ghana, cha juu ni Sh 30,000 na chini ni Sh 5,000. Akitangaza vingilio hivyo, Ofisa Uhusiano wa Yanga, Jerry Muro alisema vingilio vingine ni Sh 20,000 na Sh 7,000.Pia alisema kukosekana kwa Ngoma na Kamusoko si tatizo na kwamba kocha ameshafanyia kazi suala hilo na mashabiki wasiwe na hofu, Yanga ina wachezaji wengi wenye uwezo mkubwa.Kwa upande wake, Pluijm alisema amewapanga vyema vijana wake na kuwaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono katika mchezo huo. “Tupo vizuri, tumejipanga kwa ajili ya kuwapa furaha mashabiki wetu,” alisema Pluijm.
4
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, Simba leo wanashuka dimbani kuwakabili Coastal Union ya Tanga katika mchezo wa ligi hiyo utakaochezwa kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Mchezo huo ni muhimu kwa Simba kama itashinda itafikisha pointi 81 katika michezo 31 na kuishusha Yanga iliyokaa kwa muda mrefu kileleni mwa msimamo ikiwa na pointi 80 katika michezo 34 iliyocheza. Wekundu hao wanapewa nafasi kubwa ya kushinda mechi hiyo kwasababu hawajapoteza mchezo wowote kwenye uwanja wa nyumbani tangu kuanza kwa msimu huu.Timu hizo zilikutana katika mchezo wa raundi ya kwanza kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga, na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1. Mwenendo wao kwenye ligi hivi sasa ni kama hawakamatiki kutokana na ubora wa kikosi chao kuanzia safu ya ushambuliaji inayoongozwa na Meddie Kagere anayeongoza kwa mabao 17, John Bocco 14 na Emmanuel Okwi 11.Mpaka sasa unaweza kusema Simba ni bora zaidi kwenye ushambuliaji ikiongoza kwa kufunga mabao 61 ikifuatiwa na Yanga yenye mabao 54. Lakini pia, safu ya ulinzi iko vizuri kwani imefungwa mabao 12 kwenye nyavu zake ikiwa ndio timu pekee yenye mabao machache. Coastal Union inayoshika nafasi ya 10 kwenye msimamo, imeshacheza michezo 33 na ina pointi 41.Timu hiyo licha ya kuonyesha ushindani katika baadhi ya mechi zao zilizopita inaonekana kuwa na mapungufu kwenye safu ya ulinzi ikifungwa mabao mengi 33 kuliko mabao iliyofunga wao 29. Ni timu inayoonekana kucheza kwa kulinda na kushambulia kiasi kwani sare walizopata ni 14.
4
Walter Mguluchuma -Katavi WAKAZI wa Mtaa wa Kilimahewa, Manispaa ya Mpanda, jana walikumbwa na taharuki baada ya kuvamiwa na nyati na kulazimika kujifungia ndani  ya nyumba zao. Mwenyekiti wa mtaa huo, Cristophar Masumo,   alisema tukio hilo lilionekana kuwapa mshtuko wananchi, huku wanafunzi wakishindwa kwenda shule. Alisema tukio hilo lilitokea jana saa 2 asubuhi Mtaa wa Kilimahewa jirani na Shule ya Sekondari Shanwe. Mmoja wa wakazi wa mtaa huo, Lina Philemon,  alisema alikuwa akiosha vyombo nyumbani kwake, akafuatwa na jirani yake na kumwambia amemwona ng’ombe  amelala  jirani na  nyumba yake. Alisema kuwa hali hiyo ilimfanya atoke nje kwenda kutazama, lakini akiwa bado anashangaa, jirani mwingine alipiga yowe na kumwambia akimbie atakufa kwa sababu huyo si ng’ombe. “Nililazimika kurudi ndani ya nyumba yangu na kujifungia ndani na familia yangu tukipiga yowe kuomba msaada,” alisema.  Naye Rose David alisema yeye aliona umati mkubwa wa watu wakikimbia ovyo, huku wakipiga yowe kuomba msaada. Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Shanwe, Salaphina Pikilini anayesoma darasa la sita, alisema tukio hilo lilitokea wakati akiwa anakwenda shule na mwenzake, walimwona nyati huyo, lakini hawakutambua kama ni mnyama hatari. “Wakati tunaulizana na wenzangu, yule mnyama alinyanyuka na kuanza kutufuata upande wetu, tulikimbia kasi kujiokoa,” alisema.  Askari wa Maliasili walifika na kukuta watu wamejifungia ndani ya nyumba zao, huku nyati akiwa anazunguka zunguka eneo hilo. Walimpiga risasi mbili ambazo hazikumpata vizuri, hadi mkazi wa eneo hilo, Bila Yusuph aliyekuwa na bunduki yake kumpiga risasi tatu zilizompata. Baada ya kuuawa nyati huyo, wananchi walifurika eneo la tukio wakiwa na mapanga na visu kupata kitoweo .  Kutokana  na umati mkubwa, askari wa Maliasili na wale wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji walilazimika kuwatawanya, kisha kumchukua nyati hadi ofisi za maliasili ambako waligawana watumishi wa Serikali tu.
3
  CHRISTINA GAULUHANGA NA VERONICA ROMWALD-DAR ES SALAAM   SAMAKI wanaovuliwa katika Bahari ya Hindi sasa kuuzwa katika mabucha maalumu ya asamaki badala ya mitaani kama ilivyo sasa. Akizungumza na MTANZANIA ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Uvuvi wa Soko hilo, Victoria Mwandike alisema uongozi wa soko hilo uko kwenye mchakato wa kupendekeza hatua hiyo ili kuzuia uuzwaji holela wa samaki wapo samaki wanaouzwa mitaani hasa kwenye vituo vya mabasi na mitaani. Pamoja na mambo mengine alisema zaidi ya tani 1.5 waliovuliwa kwa njia ya milipuko na baruti wamekamatwa katika soko la Kimataifa la Samaki Feri jijini Dar es Salaam. Samaki hao walikamatwa wiki iliyopita katika msako maalumu kabla ya kuanza kusambazwa kwa wafanyabiashara kwa ajili ya kuuzwa. “Bado tunafanya msako wa kukamata na kudhibiti uingizwaji wa samaki waliovuliwa kwa njia haramu, wiki iliyopita zilikamatwa tani 1.5 na mapema wiki hii tumekamata kilo 20,” alisema. Alisema kutokana na hali hiyo bado wanahimiza Watanzania kuwa makini kwani wavuvi hao wasiokuwa waaminifu wanaendelea kuingiza samaki hizo. “Lakini kwa kuwa tunaimarisha mifumo yetu ya ndani ya soko sasa wanawauzia wafanyabiashara na wao wanakwenda kuwauza moja kwa moja huko mitaani, wavuvi waliokamatwa na maofisa hao tayari wamechukuliwa hatua za kisheria. “Lakini ni vema sasa mamlaka zinazohusika na uuzwaji na usimamizi wa milipuko hasa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Wizara ya Kilimo na Mifugo na Jeshi la Polisi wadhibiti upatikanaji holela wa bidhaa hiyo ili tutokomeze uvuvi haramu ambao kwa sasa umekithiri katika Bahari ya Hindi,” alisema. Alisema wavuvi baada ya kununua milipuko hiyo huipooza kwa kuchanganya na kemikali wanazozifahamu wao kisha huitumia kwa kuvua samaki. “Zipo athari nyingi za uvuvi haramu lakini kikubwa eneo hilo hupoteza uhalisia wake kwa zaidi ya miaka 100  na baada ya hapo ndiyo huanza kurejea katika hali ya kawaida, jambo ambalo limesababisha hata samaki siku hizi samaki kupatikana maeneo ya mbali tofauti na zamani,”alisema Mwandike.
3
 PENNSYLVANIA, MAREKANI MAUAJI ya raia wa China, mtafiti wa masuala ya virusi vya corona kwenye ardhi ya Marekani, yamesababisha nadharia mbalimbali duaniani kuwa kuna sababu iliyojificha kuhusu kifo chake.  Bing Liu, profesa msaidizi mwenye miaka 37 katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Pittsburgh, Marekani alikutwa amefariki dunia nyumbani kwake Jumamosi iliyopita. Wenzake walisema alikuwa karibu kupata “matokeo muhimu” ya tafiti kuhusu Covid-19, tukio lililosababisha kuwepo kwa maoni mitandaoni yanayoeleza kuwa yawezekana Liu aliuawa lakini polisi walisema ni tukio la kujiua.  Kwa nini Liu aliuawa? Kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo, mtafiti huyo alikutwa katika makazi yake eneo la Pittsburgh akiwa na majeraha mengi ya risasi kichwani, shingoni  Mtu aliyekuwa na silaha alitambulika kuwa na miaka 46, mhandisi wa programu ya kompyuta, Hao Gu. Mamlaka zinasema muuaji naye alijiua baada ya kurudi kwenye gari lake. Liu na Gu walikuwa wanafahamiana, maofisa wapelelezi wa mauaji walieleza. Uchunguzi umebaini kuwa lilikuwa tukio la kuua na kujiua lililotokana na mgogoro wa muda mrefu wa masuala ya kimapenzi. ‘’Hakuna ushahidi wa kuhusisha tukio hilo na utafiti wa Liu na mazingira ya sasa ya changamoto za kiafya,”walisema wapelelezi hao.  Liu ni nani?  Katika taarifa yao wenzake wamemwelezea kama mtafiti wa kipekee ambaye alikuwa ukingoni kufanikisha kupata matokeo muhimu ya kuelewa maambukizi ya Covid-19.  Waliomboleza kifo cha Liu na kuahidi kumalizia utafiti wake zikiwa ni juhudi za kuenzi ubora wake katika uwanja wa kisanyansi. Liu, ambaye ni raia wa China alipata shahada yake ya kwanza na shahada ya uzamivu katika masomo ya sayansi ya kompyuta nchini Singapore kabla ya kufanya utafiti nchini Marekani. Aliwahi kuungana na wanabaiolojia wengine kufanya utafiti kuhusu kinga ya binaadamu, kwa mujibu wa wasifu wake mtandaoni. 
2
Azam ilikuwa na uwezo wa kuongoza ligi kama ingeshinda mchezo wa jana, lakini sare imeifanya ilingane pointi na Yanga na izidiwe idadi ya mabao ya kufunga ambapo Yanga imefunga sita na Azam matano.Mabao ya Yanga jana yalifungwa na Obrey Chirwa dakika ya 39 na Ibrahim Ajibu dakika ya 47 huku kila mmoja akimchangia mwenzake pasi la bao. Bao la kufutia machozi la Kagera likifungwa na Jaffar Kibaya dakika ya 52.Hata hivyo, kuendelea kukaa kileleni kwa Yanga kunategemea matokeo ya mechi ya Simba na Mtibwa Sugar leo ambapo zote zina pointi 11 hivyo timu itakayoshinda itaongoza na endapo zitatoka sare ina maana zitaungana na Yanga na Azam kwenye pointi 12 na mwenye uwiano mzuri wa mabao ndiye atakayekaa kileleni.Kagera Sugar inaendelea kushika mkia kwa pointi mbili baada ya kupoteza michezo minne na kupata sare mbili ikiwa haijashinda mchezo hata mmoja. Michezo mingine iliyochezwa jana ni Singida United iliyopata suluhu ugenini Uwanja wa Mabatini dhidi ya Ruvu Shooting, Ndanda FC ilitoka sare ya bao 1-1 nyumbani Nangwanda Sijaona dhidi ya Majimaji.Kikosi cha Kagera Sugar: Juma Kaseja, Mwaita Gereza, Adeyoum Ahmed, Juma Shemvuni, Juma Nyosso, Ally Iddi, Venence Ludovic, Ozuka Okochukwu, Jaffar Kibaya, Omar Daga na Christopher Edward/Themi Felix.Yanga SC: Youthe Rostand, Juma Abdul, Gardiel Michael, Andrew Vincent, Kelvin Yondani, Said Juma ‘Makapu’/Raphael Daudi, Pius Buswita, Papy Tshishimbi, Obrey Chirwa/Maka Edward, Ibrahim Ajib, Geoffrey Mwashiuya/Emmanuel Martin
4
MECHI ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon 2019) kati ya Tanzania na Uganda imesogeza mbele Mkutano Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Pwani Corefa na sasa utafanyika Machi 31.Akizungumza na jana Mwenyekiti wa Corefa, Hassan Hassanoo alisema wameamua kupeleka mbele mkutano huo wa mwaka uliopangwa kufanyika Jumapili, Machi 24 ili kwenda kuisapoti timu hiyo ya Taifa, ambayo itacheza dhidi ya Uganda Cranes kusaka nafasi ya kufuzu kucheza fainali za Afcon 2019 nchini Misri. “Tumesogeza mbele Mkutano Mkuu kwa lengo kubwa moja ya kuipa nafasi mechi ya Taifa Stars dhidi ya Uganda ili kunesha uzalendo wetu kwa taifa ili kuhakikisha timu yetu inashinda mchezo huo,” alisema Hassanoo.Aidha, alisema baada ya mchezo huo watahakikisha mkutano wao unafanyika Machi 31 kama walivyopanga huko Rufiji na kuwataka wadau na wapenzi wengine wa soka kuwaunga mkono. Alisema kuwa wanaitakia kila la heri Taifa Stars ili kushinda pambano lake hilo la Jumapili dhidi ya Uganda, ambao tayari wameshafuzu kwa fainali hizo nchini Misri. Katika mchezo wa kwanza, Udanda Cranes ilitoka sare na Taifa Stars kwenye Uwanja wa Nelson Mandela jijini Kampala.
4
Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora imesema, Jukwaa la Fursa za Biashara litakalofanyika mjini Tabora ni fursa nzuri ya kukuza uchumi wa wananchi kwenye wilaya hiyo.Mkurugenzi Mtendaj wa Halmashauri hiyo, Martha Luleka amesema ofisini kwake kuwa, jukwaa hilo litakalofanyika Nvemba 21 hadi 23 litawezesha watu wa ndani na nje ya Tanzania kuzifahamu fursa zilizopo ili wazitumie kwa manufaa yao na ya wananchi wa Sikonge."Kwa bahati nzuri tumejaliwa kuwa na Mkuu wa Mkoa Mheshimwa Aggrey Mwanri ambaye anaweza, ana uwezo wa kuufahamisha umma wa Tanzania na nje ya nchi kuhusu uwezo au nafasi ambayo Tabora iko tayari kuitoa kwa wananchi wengine walioko ndani na nje ya nchi kuweza kuja kunyakua fursa zilizopo katika mkoa wetu” amesema wakati akizungumza na timu ya wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) waliokwenda Sikonge kuzitangaza fursa zilizopo huko.Luleka amesema, kuna mambo makubwa mawili yaliyosababisha Mkoa wa Tabora uamue kuwa na Jukwaa la Fursa za Biashara likiwemo la kupanua biashara na uwekezaji kwa wananchi wa Sokonge.“Lakini Sababu ya pili nayo ni nzito sana ni kwamba tunaandaa kukaribsha uwekezaji mpya. Kwa nini uwekezaji mpya, wale wawekeza watakaokua wamekaribishwa kuja kwenye jukwaa hili ndipo watakapokutana na sisi wenyeji wa hizi wilaya mbalimbali au halmashauri mbalimbali kuelezeakwa ufasaha zaidi nini kilichopo katika Halmashauri zetu katika namna ya fursa za biashara na fursa za uwekezaji” amesema.Luleka amesema, halmashauri ni vituo vikubwa vya uwekezaji kwenye mkoa wa Tabora na kwamba, unapozungumzia halmashauri una maana ya kata.“Kwa mfano Sikonge tuna kata ishirini…hivi kwetu sisi ndio vituo vikubwa vya mapato ya halmashauri. Ukisikia tuna mapato ya ndani na ukisikia Mheshimiwa Jafo anasisitiza kwamba kila halmashauri isishke chini ya asilimia themanini ya mapato ya makusanyo tunaowategemea ni kata hizi. Kata zikifanya vibaya hatufiki asilimia themanini kwa maana gani kwamba kwenye kata ndio kuna pesa” amesema.
5
MABALOZI wa Tanzania wanaowakilisha nchi katika mataifa mbali mbali duniani, wamempongeza Rais John Magufuli kwa kuamua na kutekeleza mradi mkubwa wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere katika maporomoko ya mto Rufiji, huku wakiwakemea wanaopotosha mradi huo.Mabalozi hao zaidi ya 40 wametembelea mradi huo juzi ndani ya Pori la Akiba la Selous wilayani Rufiji mkoani Pwani, na walionekana kuwa na shauku kubwa wakati wakipewa maelezo ya mradi na wakati walipotembelea baadhi ya maeneo ambayo tayari kazi inaendelea kufanywa na wakandarasi.Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Dk Emmanuel Nchimbi alisema mwenye akili anaona mambo makubwa, yanayofanyika Rufiji ya mradi huo mkubwa, na kuipongeza Serikali ya Rais Magufuli kwa kuamua kuutekeleza mradi huo utakaofua megawati 2,115 utakapokamilika Juni mwaka 2022.“Serikali imedhamiria kwenda kwenye uchumi wa viwanda na sijui nitumie lugha gani, viwanda vya uhakika vinahitaji umeme wa uhakika. Wanaopinga mradi huu usitekelezwe wanataka tuwe maskini hadi mwisho wa dunia,” alisema Balozi Dk Nchimbi.Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki alieleza kuwa mradi kama huo wa Bwawa la kufua umeme la Three Gorges nchini China ulipigwa vita wakati ukianza kutekelezwa lakini sasa unapigiwa mfano kote duniani, hivyo Tanzania ina kila sababu ya kutekeleza mradi wa Julius Nyerere Hydro Power Project (JNHPP).“Mradi huu utakuwa na manufaa makubwa kwa Watanzania, hatuna budi kuutekeleza ili kufikia Tanzania ya viwanda. China walipoanza mradi wao wa Three Gorges walipigwa vita sana, lakini nasi hatuna budi kuukamilisha mradi wetu. Utatuletea matokeo chanja sana,” alisema Balozi Kairuki.Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Dk Wilbrod Slaa alisema mradi huo ni ukombozi kwa Watanzania kiuchumi na kumpongeza Rais Magufuli kwa kusimama kidete kuhakikisha unatekelezwa licha ya kelele za baadhi ya watu.“Mradi huu utaondoa tatizo la umeme ambalo limekuwa likitukabili muda mrefu. Lakini ni mkombozi katika Tanzania ya uchumi wa viwanda. Naipongeza serikali kwa hatua hii kubwa, msingi wa tanzania ya viwanda umepatikana,” alisema Dk Slaa.Aidha, aliongeza kuwa uzalishaji huo wa megawati 2,115 usiwe ndio mwisho wa kusaka nishati zaidi, na kwamba pamoja na nishati ya umeme ya sasa megawati takriban 1,600, nchi ilenge kufikia azma iliyosemwa ya kuwa na megawati 10,000 ifikapo mwaka 2025 ili kuwa na uhakika mkubwa zaidi wa nishati.Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Dk Abdallah Possi alisema mradi huo utaingia katika historia kwani bwawa hilo litakalokuwa na maji mita za ujazo bilioni 33.2, litakuwa miongoni mwa mabwawa makubwa 70 duniani.“Lakini zaidi utasaidia katika suala uhifadhi wa mazingira kwani tumeona jinsi mazingira yanavyoathirika kwa ukataji wa miti kwa shughuli mbali mbali zikiwamo za kuni, ambako Jiji la Dar es Salaam ni mtumiaji mkubwa wa nishati hiyo,” alieleza Dk Possi.Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya mabalozi wenzake baada ya kutembelea mradi huo, Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Wilson Masilingi alisema ziara hiyo imewafurahisha sana, na wanakwenda kutangaza fursa za mradi huo kwa wawekezaji ambao watahitajika katika masuala ya teknolojia ya mitambo itakayojengwa.“Tumepewa heshima kubwa sana kutembelea mradi huo na tumefurahishwa mno kuja hapa. Tumeona kazi kubwa na nzito inayofanyika, katika mazingira magumu lakini yamefanywa kuwa mepesi, tunawapongeza sana,” alisema Balozi Masilingi.“Tunakwenda kwenye mataifa yetu tunayowakilisha, kuwatafutia teknolojia sahihi, kwa mataifa sahihi na kwa ushindani safi, lakini kwa kuhakikisha ninyi wataalamu ndio mnaamua kwa utaalamu wenu bila kubanwa na yeyote, kwani mnafanya kitu kizuri kwa niaba yetu na kwa niaba ya Watanzania,” aliongeza.Awali, Mratibu wa Mradi wa JNHPP, Stephen Manda aliwaeleza mabalozi hao kuwa licha ya kelele za baadhi ya watu, mradi huo utatekelezwa kwa manufaa ya Watanzania, na hadi sasa unakwenda vizuri kwa mujibu wa mkataba na makandarasi kampuni za ubia za Arab Contractors na Elsewedy Electric zote za Misri.Manda alisema kwa sasa wameshajenga baadhi ya madaraja ya muda katika mto Rufiji na hivi sasa wameshachimba mtaro handaki kuchepusha maji katika eneo, ambalo litajengwa bwawa hilo litakalokuwa la kwanza Afrika Mashariki kwa ukubwa, na la nne katika Afrika.Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Juma Njwayo aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo, aliwaambia mabalozi kuwa mradi huo unatekelezwa katika eneo la takriban asilimia mbili tu ya eneo lote la kilometa za mraba 50,000 za Pori la Akiba la Selous, hivyo kelele zinazopigwa na baadhi ya watu na mataifa ni upotoshaji ambao mabalozi hao wanapaswa kuukemea. Aliwataka wamuombee Rais Magufuli ili aendelee kusimamia mradi huo na miradi mingine ya maendeleo.
3
SERIKALI imetaka wakuu wa shule za sekondari na vyuo vikuu mkoani Kilimanjaro, kuandaa utaratibu maalumu ambapo wahitimu wa taaluma mbalimbali, hawatatunukiwa vyeti vyao bila kwanza kupanda Mlima Kilimanjaro.Mpango huo umelenga kuhamasisha utalii wa ndani lakini pia kuongeza mapato, jambo ambalo litasaidia uimarishwaji wa miradi ya kijamii hususan vijiji vinavyozunguka mlima huo.Mkuu wa Mkoa huo, Anna Mghwira alisema hayo jana wakati akizindua kampeni ya kupanda mlima huo kama sherehe za miaka 57 ya Uhuru wa Tanzania zenye kaulimbiu, ‘Ujasiri na uzalendo, dira ya kuimarisha utalii Tanzania’.Akizungumza kwa niaba ya Mghwira, Mkuu wa Wilaya ya Siha, Onesmo Buswelu alisema serikali itaandaa mazingira rafiki kusaidia kutekelezwa kwa mpango huo kwa mafanikio.“Leo tunashuhudia timu ya watu 40, wakiwemo wanajeshi kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Watumishi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), wanahabari na watendaji wa Taasisi ya Benjamin Mkapa na Umoja wa Ushirikiano baina ya Tanzania na China, wanapanda mlima huu,” alisema.Alisema endapo mpango huo wa shule za sekondari na vyuo hivyo wa kupanda Mlima Kilimanjaro utaanzishwa utasaidia kujenga uzalendo na ujasiri kulinda rasilimali za Taifa.Katika safari hiyo iliyoratibiwa na Tanapa kwa kushirikiana na Kampuni ya kupandisha Watalii Mlima Kilimanjaro ya Zara, na kupanda mlima kupitia njia ya Marangu, Mghwira alitaka wadau zaidi kuunga mkono juhudi za serikali. Alitaka viongozi waliopewa dhamana ya kulinda rasilimali za Taifa kufanya kazi hiyo kwa uzalendo na kuwa na mikakati ya kuzilinda.Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Tanapa, Jenerali mstaafu, George Waitara alisema mpango kupanda mlima huo ulianza mwaka 2008 na lengo ni kuhamasisha utalii wa ndani na utunzwaji wa mazingira na maliasili za Taifa. “Awali wakati naongoza kampeni ya kupanda mlima huu sikuwa nafahamu kama nitakuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tanapa. Nimebaini tunahitaji uzalendo na ujasiri katika kulinda rasilimali za Taifa, kinyume na hapo rasilimali hizi zitapotea na dunia itatushangaa,” alisema.
3
Wamesema hatua hiyo itaongeza mitaji, pia kutoa hamasa kwa wanachama kupata mikopo mingi zaidi itakayowasaidia katika shughuli za kiuchumi.Meneja wa Saccos hiyo, Abbas Rajab akisoma taarifa ya Saccos kwa Rais Jakaya Kikwete, jana kabla ya kuizindua, alisema Saccos hiyo yenye wanachama 1,779 kati ya hao wanawake wakiwa ni 500 imefanikiwa kuwa na mtaji wa Sh bilioni 4.3 na mikopo iliyokopeshwa na kurejeshwa ni Sh bilioni 3.3 , wakati mikopo ya kiasi cha Sh bilioni 1.04 haijarejeshwa na wanachama.Kwa mujibu wa meneja huyo chama kinajiendesha chenyewe bila kutegemea mikopo kutoka nje na kwamba hadi sasa kina mtaji wa Sh bilioni 1.4 zikiwa ni akiba, amana na limbikizo la ziada.Hata hivyo, alisema kutokana na hayo, Saccos hiyo imepata mafanikio kupunguza kero mbalimbali za kiuchumi na kijamii na kutengeneza ajira kutokana na wanachama wake kununua magari 100, pikipiki 150 na kufungua maduka.Kwa mujibu wa meneja huyo kuna changamoto kubwa kwa baadhi ya wanachama kutorejesha mikopo kwa wakati na tozo la kodi kubwa ya TRA ya asilimia 30 na kumwomba Rais kuwapatia majawabu ombi hilo.Kwa upande wake, Rais Kikwete, kabla ya kujibu hoja hizo, aliwapongeza wananchi hao kwa kuanzisha Saccos ambayo inajitegemea kimtaji na kukopesha wanachama wake fedha nyingi.Rais alisema utaratibu wa kuanzisha Saccos lilikuwa ni jambo zuri kwa kuwa ni chombo kinachoweza kumkomboa mwananchi wa kawaida kwani mabenki si rafiki wa watu masikini.“Vyama hivi vimeanzishwa ili kumkomboa mtu wa chini kwani mabeki si rafiki yao na Saccos zina faida ya kuwawezesha wanachama kujikopesha kwa ajili ya maendeleo yao ya kukuza uchumi wa mtu moja mmoja na taifa,” alisema Rais.Katika hotuba hiyo alikubali ombi lao kwa kuwapatia kompyuta hizo tatu na kuwasihi wanachama kujenga tabia ya kurejesha mikopo kwa wakati ili wanufaishe na wenzao.
5
KATIBU Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) Godfrey Mngereza ame- sema Tamasha la Utama- duni la Afrika Mashariki (JAMEFEST) limetoa elimu na kuwanufaisha watu wengi kiuchumi na kisiasa. Akizungumza na gazeti hili Mngereza alisema mbali na wajasiriamali waliotumia fursa kuuza bidhaa zao pia, kuna hoteli na watu wa usafiri na utalii lakini pia Mama Ntilie walionufaika kupitia wageni mbalimbali kutoka nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.“Wengi wamenufaika tumeona bidhaa mbalimbali, watu wameuza kupitia tamasha, kuna watu wa tax, bodaboda ambao wamepata wateja, kuna vikundi vya wasanii navyo vimetumikia jukwaa kujitangaza pia, “alisema. Mngereza alisema alichokifurahia zaidi ni kuona makundi tofauti yameshirikishwa waki- wemo watu wenye ulemavu, ambao wameonesha uwezo mkubwa katika ubunifu wa sanaa za mikono hali iliyovu- tia kununua bidhaa zao. Alisema kwa kile alichokiona anahimiza umuhimu wa jamii ku- towafungia watoto wenye ulemavu ndani badala yake wafundishwe sanaa za mikono ziwasaidie kujik- wamua kiuchumi. “Naamini kabisa wenye ulemavu kutokana na uwezo wao wakifundishwa sanaa za mikono wanaweza kufanya mambo makubwa, jambo la muhimu wasiwa- fungie watoto ndani kwa kuona aibu, wawatoe na kuwaelimisha watafanikiwa kiuchumi, “alisema. Katibu huyo alisema ku- pitia tamasha watu wameb- adilishana uzoefu, wame- jenga mtandao, wamejifunza tamaduni za kila nchi hivyo, ushirikiano huo wa Jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki utaendelea kudumu na kuimarisha uchumi wa nchi hizo.
4
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa onyo kali kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, Geoffrey Mwangulumbi na Mweka Hazina wa manispaa hiyo, Pascal Makoye kuwa anawataka wabadilike na waache kugombana na badala yake watekeleze majukumu yao ipasavyo.Pia, amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack azisimamishe kazi kampuni zote zilizopewa zabuni ya kukusanya mapato katika manispaa hiyo, kwa kuwa zimeshindwa kufanya kazi vizuri na zina madeni. Alitoa maagizo hayo jana wakati alipozindua nyumba 10 za askari Polisi katika Manispaa ya Shinyanga eneo la Kambarage.Mradi huo umetokana na Sh milioni 225 zilizotolewa na Rais John Magufuli. Waziri Mkuu alisema viongozi hao wameshindwa kutekeleza majukumu yao, ikiwemo kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato na kutoa kazi hiyo kwa kampuni zisizokuwa na uwezo. Alisema mwaka jana walikadiria kukusanya Sh milioni 800 na badala yake walikusanya Sh milioni 500.Alisema manispaa hiyo haiwezi kusonga mbele kimaendeleo, iwapo viongozi wake hawaelewani wanagombana kila siku.“Mkurugenzi na wenzako nawaonya kwa mara ya mwisho badilikeni na hakikisheni mnatekeleza majukumu yenu ipasavyo yakiwemo ya ukusanyaji wa mapato,” alisema Waziri Mkuu.Akizungumzia kuhusu nyumba za askari Polisi, Waziri Mkuu alisema lengo la ujenzi wa nyumba hizo ni kuhakikisha askari wanaishi katika mazingira mazuri, yatakayowawezesha kutekeleza vizuri majukumu yao.“Ili waweze kutekeleza vizuri majukumu yao lazima wawe na makazi mazuri,” alisema.Pia, Waziri Mkuu alitoa wito kwa askari waliopewa funguo kwa ajili ya kuishi katika nyumba hizo, wahakikishe wanazitunza vizuri. Kwamba hata inapotokea wamehamishiwa kwenda katika vituo vingine, wale watakaohamia wakute nyumba hizo zikiwa katika mazingira mazuri.Waziri Mkuu alisisitiza kuwa ujenzi wa nyumba hizo ni endelevu, ambapo pia alizitaka idara mbali mbali za serikali, ziendelee na mchakato wa ujenzi wa nyumba zake, kwani wakiwa na nyumba nyingi itapunguza idadi kubwa ya askari wanaoishi uraiani.Awali, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Richard Abwao alisema awali fedha zilizotolewa, zilikuwa zijenge nyumba tisa za vyumba viwili, lakini kutokana na ubunifu waliboresha mradi huo, kwa kuongeza nyumba moja na kuongeza chumba kimoja, hivyo kuufanya mradi huo kuwa na nyumba 10 zenye vyumba vitatu vya kulala.Abwao alimshukuru Rais Magufuli kwa upendo wake mkubwa kwa Jeshi la Polisi Tanzania, kwa kulipatia fedha za kuboresha makazi ya askari. Mradi huo umekamilika kwa gharama ya Sh 278, 565, 500 wastani wa gharama za ujenzi kwa nyumba moja ni Sh 27, 856, 550. Alisema kiasi cha nyongeza cha Sh 53, 565,500 zilitolewa na wadau mbali mbali.
3
Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA MBUNGE wa Chemba, Juma Nkamia (CCM), amemshambulia Mkuu wa Wilaya hiyo, Simon  Odunga, mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  Jordan Rugimbana kwa madai kuwa anafanya kazi kwa ubabe. Wiki iiyopita,   Odunga alinusurika kupigwa na wananchi wa Kijiji cha Mlongia Kata ya Jangalo Tarafa ya Mondo   kwa madai kuwa alitoa lugha ya kuudhi na vitisho kwa wananchi wa kijiji hicho. Nkamia alliyasema hayo jana mjini hapa wakati akichangia katika kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa wa Dodoma (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Maendeleo Vijijini (Mipango). Mgeni rasmi katika mktano huo alikuwa ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.  Baada ya Waziri Mkuu kuufungua na kuondoka, ndipo Nkamia alipoanza mapambano ya maneno dhidi ya mkuu huyo wa wilaya. Nkamia ambaye alipewa nafasi ya kuzungumza alimuomba Mkuu wa Mkoa Rugimbana kutatua migogoro ambayo inasababishwa na baadhi ya viongozi akiwamo Odunga. Mbunge huyo alimtaka mkuu wa mkoa kuangalia uwezekano wa kutatua migogoro ya ardhi ambayo inaonekana kushamiri kwa kasi katika Mkoa wa Dodoma. “Sijui wananunuliwa na wawekezaji tena wawekezaji matapeli, nashangaa kuona kijiji kinakuwa na mamlaka ya kugawa zaidi ya ekari 500 wakati kanuni zinaonyesha kijiji kinatakiwa kugawa ekari zisizodi 50. “Ni mamlaka gani zinazompa Mkuu wa Wilaya kuhamisha mipaka… amekuwa akilazimisha kuhamisha mipaka kutoka sehemu moja kwenda nyingine bila kuwashirikisha wananchi lakini mtu akitaka kuhoji jambo lolote anawekwa ndani,’’ alisema Nkamia Mbunge huyo wa Chemba, alisema mkuu huyo wa wilaya amekuwa akiendesha shughuli zake kwa ubabe huku akijiita Rais wa Wilaya bila kujua kuwa Rais ni mmoja. Baada ya mbunge kuzungumza, Mkuu wa Mkoa, Rugimbana alikataa kumpa nafasi kuzungumza DC Odunga na kusema kuwa anaijua migogoro ya ardhi jinsi ilivyo. “Kimsingi naijua migogoro ya ardhi jinsi ilivyo hivyo tutaangalia jinsi ya kuitatua, hivyo nimewaelewa naomba tuendelee na mambo mengine. “Nitaomba wakuu wa wilaya, wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri zote tukutane kwa muda mfupi tuweze kuongea mambo machache,’’ alisema Rugimbana
3
Kessy aliyesajiliwa na Simba kwenye dirisha dogo la usajili Desemba mwaka jana akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro, alisema makubaliano yake na Simba yalikuwa ni kupewa nyumba lakini tangu aanze kuichezea timu hiyo mambo yamekuwa tofauti na amekuwa akiishi kwa jamaa jambo ambalo linamkera.“Moja ya makubaliano yetu kwenye mkataba ilikuwa ni nyumba ya kuishi na viongozi wa Simba waliahidi kunitimizia hilo, lakini kadri muda unavyokwenda naona kimya na nikiwauliza wanaonekana kutojali suala langu mbaya zaidi uongozi unaonekana kuwapa umuhimu zaidi baadhi ya wachezaji zaidi ya wengine hasa wazawa,” alisema Kessy.Kessy mwenye uwezo mkubwa wa kusaidia mashambulizi, alisema baada ya kuona uongozi unampuuza ameamua kuondoka kambini na kurudi kwao Morogoro, kuangalia mambo mengine hadi hapo viongozi wake watakapomhakikishia mahali pa kuishi pamoja na deni la fedha zake za usajili zilizobaki.Beki huyo alisema endapo atapatiwa ufumbuzi wa mambo hayo yupo tayari kurudi kazini kuendelea kuitumikia Simba kwa sababu soka ndiyo kazi yeke pekee inayomuingizia kipato cha kuendesha maisha.Naye Meneja wa mchezaji huyo, Athumani Tippo alisema, Simba walikubali kumtafutia Kessy nyumba ya kuishi, lakini anashangaa kuona wakimbadilikia mteja wake na anapowauliza majibu yanakuwa tofauti na ilivyokuwa wakati wa makubaliano.Kwa upande wake msemaji wa Simba, Haji Manara alisema mchezaji huyo hayupo kwenye kikosi kutokana na matatizo ya kifamilia, na hakuna mtu anayejua mkataba wa Kessy na Simba ukoje, hivyo inawezekana malalamiko ya Kessy yakawa hayapo kwenye mkataba.
4
['Huenda Manchester United ikasubiri ukaguzi wa mchezaji wa kiungo cha mbele raia wa Ufaransa Anthony Martial, mwenye umri wa miaka 23, kabla ya kuruhusu uhamisho wa mkopo wa mchezaji wa kimataifa wa Chile Alexis Sanchez, mwenye umri wa miaka 30, kwenda Inter Milan. (Guardian)', 'Paris St-Germain imeambia Real Madrid itatafakari kumuuza mchezaji wa Brazil wa kiungo cha mbele Neymar, mwenye umri wa miaka 27, iwapo mchezaji wa klabu hiyo ya Uhispania mwenye miaka 19 na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Jr iatakuwa sehemu ya makubaliano ya kudumu. (AS)', 'Wakurugenzi wa Barcelona wamekutana Jumatatu kujadili ombi la mchezaji wao wa zamani Neymar. (Marca)', 'Huenda Inter Milan ikamgeukia mchezaji wa kiungo cha mbele wa Manchester City Wilfried Bony, mchezaji huyo wa Ivory Coast mwenye miaka 30 kwa sasa haichezei klabu yoyote baada ya kuachiwa na Swansea msimu wa joto. (Goal.com)', 'Mchezaji wa kimataifa wa Serbia Nemanja Matic, mwenye umri wa miaka 31, ameitisha mazungumzo na meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer baada ya kuipoteza nafasi yake ya kwanza huko Old Trafford. (Mirror)', 'Arsenal ipo tayari kumruhusu mchezaji wa kimataifa wa Uhispani Nacho Monreal kujiunga na Real Sociedad wiki hii iwapo mchezaji huyo wa miaka 33 na mchezaji wa kiungo cha ulinzi ataomba kuondoka. (Sun)', 'Javi Gracia anapigania kuokoa nafasi yake kama meneja wa Watford baada ya kuanza msimu wa ligi kuu England kwa kushindwa mara tatu. (Telegraph)', 'Mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham anaelekea kupata mkataba mpya ambao huenda ukaongeza zaidi ya mara mbili malipo ya mchezaji huyo wa miaka 21 raia wa England ya £50,000 kwa wiki(Telegraph)', 'Wawakilishi wa Christian Eriksen hawatofikiria pendekezo la mkataba wa Tottenham la malipo ya £200,000 kwa wiki na mchezaji huyo wa miaka 27 ambaye mkataba wake hivi sasa unamalizika msimu ujao wa joto anatumai kupata uhamisho kwenda Uhispania. (Mirror)', 'Eriksen ni kama amejiuzulu kusalia Tottenham katika kipindi kifupii, huku ndoto yake ya kujiunga na Real Madrid au Barcelona msimu huu wa joto ikishindwa kufanikiwa. (Mail)', 'Winga wa Celta Vigo Pione Sisto, mwenye umri wa miaka 24, anakaribia kujiunga na Torino baada ya uhamisho kwenda Aston Villa kutofanikiwa. (Marca)', 'Mabingwa wa Italia Sampdoria wanataka kumsajili winga wa Swansea anayeichezea timu ya taifa ya Ghana Andre Ayew, mwenye umri wa miaka 29, kwa mkopo kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya (Star)', 'Mlinzi wa Manchester United Luke Shaw, mwenye miaka 24, huenda akawa nje kwa hadi mwezi mmoja kutokana na jeraha katika msuli wake wa paja. (Talksport)', 'Huenda Sunderland ikawasilisha ombi la pili kwa mlinzi wa Sheffield Morgan Fox, 25 hapo kesho Jumatano (Newcastle Chronicle)', 'Jurgen Klopp anaamini mbinu yake ya usimamizi inaongeza uwezekano wa yeye kwenda mapumzikoni wakati kipindi chake cha usimamizi kitakapomalizika Liverpool mwaka 2022. (Times)', 'Kevin De Bruyne ameunga mkono mchezaji wa zamani wa timu ya Manchester City , Vincent Kompany kuwanyamazisha wakosoaji na kufungua ufanisi wa nafasi yake mpya kama bosi wa Anderlecht, baada ya kujizolea pointimbili katika mechi nne za kwanza msimu huu. (Manchester Evening News)', 'TETESI ZA JUMATATU', 'Mchezaji wa kiungo cha kati wa Spurs na timu ya taifa ya Kenya Victor Wanyama amepewa mkataba wa miaka mitano kwa malipo ya £65,000- kwa wiki na Club Bruges wakati anapokaribia kukamilisha uhamisho. (Scottish Sun)', 'Kalbu ya Fiorentina katika ligi ya Serie A inajitayarisha kuwasilisha ombi kwa mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United na timu ya taifa ya Brazil Fred, mwenye umri wa miaka 26. (Calciomercato)', 'Norwich itamfukuzia kipa wa Stoke na timu ya taifa ya England Jack Butland, mwenye umri wa miaka 26, ifikapo Januari na iwapo thamani yake itashuka. (Sun)', 'Bordeaux inataka kumchukua mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal na Misri Mohamed Elneny, mwenye umri wa miaka 27, kwenda Ligue 1 kwa mkopo. (Foot Mercato)', 'Leeds inatarajiwa kuanza mara moja mazungumzo na mchezaji wa kiungo cha kati Kalvin Phillips kuhusu mkataba mpya. Mchezaji huyo wa miaka 23 anataka kulipwa £40,000 kwa wiki ili kuendelea kusalia Elland Road. (Football Insider)', 'Aliyekuwa beki kamili wa Chelsea Filipe Luis, mwenye umri wa miaka 34, amekataa ombi la Manchester City, Lyon na Borussia Dortmund msimu huu wa joto kabla ya kujiunga na Flamengo kutoka nchini anakotoka Brazil. (Globo Esporte)', 'Aliyekuwa beki wa kulia wa Leicester Danny Simpson, mwenye umri wa miaka 32, anafanya mazungumzo na klabu ya Ligue 1 - Amiens kuhusu uhamisho. (Sun)', 'Meneja wa Chelsea Frank Lampard amemkaribisha mchezaji wa kiungo cha kati wa Exeter Ben Chrisene kufanya mazoezi na klabu hiyo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 15 kutoka timu ya vijana wa timu ya taifa England alifanikiwa kucheza katika kikosi cha kwanza mwezi huu. (Sun)']
4
['Kocha wa zamani wa Arsenal Arsene Wenger anajiandaa kupata ofa ya kuwa kocha wa Bayern Munich mpaka mwisho wa msimu (Sun)', 'Kiungo wa Bayer Leverkusen Kai Havertz yuko tayari kuondoka kutoka Bundesliga.Mchezaji huyo mwenye miaka 20 anatolewa macho na Manchester United.(Marca, via Metro)', 'Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer imesema kuwa kunaweza kuwa na usajili wa wachezaji wawili , lakini klabu yake itatekeleza kazi hiyo zaidi katika kipindi cha majira ya joto. (Evening Standard)', 'Chelsea inasikilizia timu zitakazomuwania mshambuliaji Olivier Giroud, 33, na winga Pedro, wakati beki wa kushoto Marcos Alonso akipambana kuhusu kuendelea kubaki Stamford Bridge. (Telegraph)', 'Fenerbahce inataka kumsajili Pendro kwa uhamisho wa bure majira yajayo ya joto.(Takvim, via Mail)', 'Pedro pia macho yake kayaangazia China (El Dorsal - in Spanish)', 'Kiungo wa Manchester United Namanja Matic, 31, yuko tayari kuondoka mwezi Januari. (Manchester Evening News)', 'Chelsea si lazima kufanya usajili mwezi Januari hata kama marufuku ya usajili itaondolewa, amesema kocha Frank Lampard.(Talksport)', 'Mshambuliaji wa Red Bull Salzburg Erling Haaland, 19, ana mpango wa kuhamia ligi ya primia katika maisha yake ya soka, anasema baba yake. Alf-Inge Haaland. (Talksport)', 'Mashabiki wa Club Africain waichangia klabu yao mamilioni ya fedha', 'Tetesi za soka Ulaya Jumatano 06.11.2019', 'Inter na AC Milan wako kwenye mazungumzo kuhusu uwanja mpya wa mpira wenye kugharimu pauni milioni 630 ulio maili nane kutoka San Siro. (Mail)', 'Kocha wa Barcelona Ernesto Valverde bado anaungwa mkono na bodi ya klabu lakini kumekuwa na wasiwasi namna timu inavyocheza. (ESPN)', 'Mlinda mlango wa Sheffield United Dean Henderson, 22, amesema karibu ajiunge na Leeds United kabla ya kujiunga tena na Blades kwa mkopo kutokea Manchester United.(Yorkshire Post)', 'Zaidi ya 90% ya mashabiki wa Manchester United hawaridhiki na namna klabu inavyoendeshwa, kwa mujibu wa utafiti.(Telegraph)']
4
KHARTOUM, SUDAN RAIS wa Sudan, Omar al-Bashir amesema sheria kandamizi yenye utata na hali ngumu ya uchumi ndiyo vimechochea hasira miongoni mwa vijana wanaoongoza maandamano ya kumtaka aachie madaraka. Matamshi hayo ya al Bashir anayekabiliwa na maandamano ya kila mara dhidi ya utawala wake, yameonyesha mabadiliko. Awali, kiongozi huyo aliwafananisha waandamanji hao kuwa sawa na panya wanaopaswa kurejea kwenye mashimo yao. Hivyo kauli ya sasa inatoa tafsiri kuwa ni sehemu ya mkakati mpya wa kusaka maridhiano na kupunguza ghadhabu za wanaompinga. Akizungumza na wanahabari Ikulu mjini Khartoum, al-Bashir amekiri kwa mara ya kwanza kuwa sehemu kubwa ya waandamanaji ni vijana waliovunjwa moyo na hali ya uchumi ikiwamo mfumuko wa bei uliopandisha gharama za vyakula na ukosefu wa ajira. Maandamano hayo yaliyoanza Desemba 19 mwaka jana yalichochewa na kupanda  bei za vyakula, ukosefu wa fedha za kutosha kwenye  benki na matatizo mengine ya  uchumi. Hata hivyo, tangu hapo hasira zao zimeugeukia utawala wa miaka 30 wa Rais al-Bashir. Polisi wamekuwa wakitumia gesi ya kutoa machozi na katika baadhi ya matukio risasi za moto kujaribu kuyasambaratisha maandamano hayo. Pia, katika hali isiyotarajiwa, al-Bashir alikwenda mbali zaidi na kutoa ahadi ya kuwaachilia huru waandishi wa habari wanaoshikiliwa na utawala wake. Bashir amesema waandishi wote wa habari ambao wamekamatwa na kufungwa kuhusiana na ghasia za maandamano wataachiwa huru. Inakisiwa idadi ya wanahabari walio jela kuwa 16.
2
Na Abducado Emmanuel, Dar es Salaam RATIBA ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu ujao, imeonekana kuzibana timu za Simba na Yanga ambazo zitacheza mechi nyingi ugenini kwenye mzunguko wa pili tofauti na mabingwa watetezi, Azam FC. Kwa mujibu wa ratiba hiyo iliyotolewa juzi na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), inaonesha Simba na Yanga zitacheza mechi saba nyumbani kwenye mzunguko wa kwanza, huku zikicheza mechi saba ugenini mzunguko wa pili. Mabingwa watetezi wa taji hilo Azam, wao wana unafuu zaidi kwani kati ya mechi zao 13 za mzunguko wa kwanza ni mechi sita pekee watakazocheza nyumbani, huku mechi saba zilizobakia wakicheza ugenini. Lakini kwenye mzunguko wa pili, watacheza mechi saba nyumbani na sita ugenini na kuziachia hali ngumu Simba na Yanga, zitakazocheza mechi saba ugenini na sita nyumbani. Ratiba hiyo inaonyesha Yanga inayonolewa na Mbrazil Marcio Maximo, itaanza mechi yake ya kwanza ugenini kwa kucheza dhidi ya Mtibwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, huku mechi ya mwisho ikimalizia ugenini kwa kucheza na Ndanda FC. Azam yenyewe itaanzia nyumbani mechi yake ya kwanza kwa kumenyana na Polisi Morogoro iliyopanda daraja, huku ikicheza nyumbani kwenye mechi yake ya mwisho kwa kucheza dhidi ya Mgambo JKT. Simba iliyoshika nafasi ya nne msimu uliopita wa ligi, itaanzia nyumbani kwenye mechi ya kwanza kwa kukwaruzana na Coastal Union, huku ikimalizia ugenini mechi ya mwisho kwa kupambana na JKT Ruvu. Ligi hiyo inayotarajia kuanza rasmi Septemba 20 mwaka huu, itasimama kwa siku 26 baada ya mechi ya raundi ya tisa zitakazofanyika Novemba 16 mwaka huu, kupisha michuano ya Kombe la Chalenji na Kombe la Uhai, itaendelea tena Desemba 20 mwaka huu.
4
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
NI shabiki gani wa kweli wa Bongo Fleva asiyemjua msanii Darassa? Ni mdau gani asiyeijua ngoma yake ya Muziki? Bila shaka wengi wanamuelewa vema huyu jamaa. Darassa mwishoni mwa mwaka jana alionyesha kuwa msanii anayeweza asifurukete kwa mwaka mzima, lakini mwishoni akamaliza vizuri. Alidhihirisha kuwa muziki pamoja na mambo mengine ni kufanya tafiti na kucheza na akili za mashabiki. Ngoma yake Muziki ilidhihirisha kuwa mwanamuziki anaweza akabadilika na kuwashika mashabiki wa rika zote kwa wakati mmoja. Darassa alifanikiwa pasi na shaka kuwaunganisha Watanzania. Ngoma yake ikawa gumzo na kwa kweli ikawa kama wimbo wa Taifa, kutokana na kukubalika kwake na kupigwa kila mahali. Ukienda baa unakutana nao, ukienda club habari ni Muziki na hata unapokuwa kwenye vyombo vya usafiri, wimbo uliopigwa zaidi ulikuwa ni Muziki. Mpaka sasa Muziki bado unabamba sehemu mbalimbali za nchi yetu na hata nje ya nchi. Ngoma yenyewe inapagawisha zaidi kutokana na midundo yake na mashairi mazuri. Kiukweli Darassa hajawahi kutoa ngoma ikaheat kwa kiasi kikubwa namna hiyo kama Muziki.Baada ya kimya cha muda mfupi, akiuacha wimbo huo uendelee kupeta mitaani, Darassa hivi karibuni ameachia ngoma nyingine. Kibao hicho kinachokwenda kwa jina la Hasara Roho, kimeonekana kufanana kwa kiasi kikubwa sana na Muziki. Ingekuwa ameimba msanii msanii mwingine, tungesema bila kupepesa macho kuwa amemkopi Darassa kila kitu. Lakini sasa kwa vile ni Darassa mwenyewe, hapa tunasema kuwa Darassa amekopi kazi yake mwenyewe na kupesti kwenye wimbo mwingine. Midundo na sauti, havina tofauti yoyote na Muziki. Inawezekana kuna udhaifu sehemu kadhaa kwa Darassa na hasa utunzi wa mashairi na washauri wa awali – maana inapaswa kabla ya msanii kuachia ngoma yake ni vema awe na watu watakaosikiliza kwanza kabla ya kuachiwa. Huenda hapakuwa na watu wa namna hiyo na kama walikuwepo walimshauri vibaya Darassa. Huko kwenye mitandao ya kijamii wadau wengi wametoa maoni yao wakieleza masikitiko yao kuhusiana na mfanano huo usio wa kawaida wa vibao vyake hivyo. Vyovyote iwavyo, Hasara Roho hauwezi kufurukuta mbele ya Muziki ambao bado unaonekana kuwa bora mpaka sasa. Ushauri wangu wa mwisho kwa Darassa, akubali kushauriwa. Ikiwa ana udhaifu wa kuandika mashairi, basi awape wenye uwezo huo wamsaidie. Kuteleza siyo kuanguka, Waswahili wamesema. Lakini pia kuanza upya siyo ujinga. Bado Darassa ana nafasi ya kufanya ngoma nyingine kali itakayorudisha heshima iliyopunguzwa na Hasara Roho. Hakuna kinachoshindikana kwa Darassa maana kama ni sauti anayo.
1
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu mstaafu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovic Utouh amesema ripoti ya CAG ndio jicho la wananchi hasa linapokuja suala la usimamizi wa rasilimali.Alisema hayo jana mjini Dodoma wakati wa warsha ya Wakurugenzi wa Asasi za Kiraia (Azaki) Kanda ya Kati inayojadili ripoti ya CAG kwa mwaka 2017/ 2018.Utouh ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wajibu alisema ripoti hiyo ni muhimu kwani ndiyo jicho la mwananchi pale linapokuja suala la usimamizi wa rasilimali kwani ripoti hiyo inaeleza mapato yaliyokusanywa, bajeti inavyoendeshwa na inatekelezwaje.Alisema kuna ripoti nne ikiwemo ya Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, mashirika ya umma na miradi na ripoti hizo zinapowasilishwa bungeni zinakuwa taarifa za wazi na wananchi wanaweza kuzipata.Alisema kutokana na ripoti za uwajibikaji za mwaka 2015/16 na 2016/17 kwa kushirikana na wadau mbalimbali ikiwemo Azaki, waliweza kutimiza utekelezaji wa mapendekezo ya CAG.Pia, alisema ili kuwepo na uwajibikaji lazima kuwepo na uadilifu na uzalendo mambo ambayo kwa miaka ya hivi karibuni yamepungua sana.“Ukiwa muadilifu unaongeza uwajibikaji wako na wote tuna jukumu la kuongeza uwazi na uwajibikaji katika kazi,” alisema.Akifungua warsha hiyo Mwenyekiti wa Mtandao wa asasi za Kiraia mkoani Dodoma (NGONEDO), Sarah Mwaga alisema asasi zimekuwa zikichochea shughuli za maendeleo na kuchochea uwazi na uwajibikaji.Alisema baada ya ripoti ya CAG kupitishwa na Bunge na sasa ni taarifa ya wazi wanajamii wanatakiwa kuifanyia tathimini Ili kuiboresha kwa maendeleo ya taifa.“Wananchi wa vijijini si rahisi kupata taarifa hizi na hawafahamu zina maana gani, wanatakiwa kujua kodi ya Serikali imekusanywaje na imepatikanaje” alisema Alisema ripoti hiyo inajadiliwa katika lugha na mfumo mwepesi Ili wananchi wapate uelewa.Kwa upande wake, Ofisa Mfawidhi Kitengo cha kujengwa uwezo wa Asasi, kutoka Foundation for Civil Society (FCS), Nasim Losai alisema warsha hiyo inakutanisha Wakurugenzi Ili kuzungumza na kuja na fikra mbadala.Pia alisema kuna ulazima kwa Asasi za Kiraia kuwa makini kutokana na suala la maombi ya ruzuku kuhusishwa na masuala ya rushwa jambo ambalo halileti picha nzuri.
3
  Na ASHA BANI-KIBAHA WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeeleza mikakati yake ya kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wenye malengo ya kukuza Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) itakayosaidia kuzalisha wataalamu bora zaidi. Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Leonard Akwilapo alitoa kauli hiyo   Kibaha jana wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Matumizi ya Tehama katika Shule za Sekondari (ADSI) utakaogharimu zaidi ya Sh bilioni nne. Alisema lengo la kusisitiza miradi ya TEHAMA ni kuendelea kuzalisha wataalamu bora zaidi katika kuelekea uchumi wa viwanda. Alisema dira ya Serikali ni kuifikisha nchi katika uchumi wa viwanda, hivyo jukumu lao ni kuwaandaa wataalamu mbalimbali  watakaokuwa wakisimamia na kuhudumia viwanda hivyo na kuongeza tija kwa taifa zima. Alisema mradi huo wa ADSI, utajikita zaidi katika kujifunza kufundisha TEHAMA katika  shule za sekondari na kwa kuanzia zimechaguliwa shule 40 katika mikoa ya Pwani na Morogoro. Alisema serikali Itahakikisha mradi huo unakuwa endelevu na katika mikoa mingine. TEHAMA ni nyenzo muhimu katika dunia ya mawasiliano, na kwa sasa ndiyo nyenzo kuu ya utoaji na usambazaji wa taarifa kwa umma, alisema. Aliwataka wadau wote wa elimu kuhakikisha wanafikisha stadi hizo katika ngazi za chini pia. Meneja Mradi wa ADSI, Joyce Msolla alisema   mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, TAMISEMI na shirika lisilo la kiserikali  la Global E-Schools and Communities Initiative (GESCI). Alisema  mradi huo utaangalia mpango endelevu wa  jumla wa shule, mafunzo ya walimu kazini, wanafunzi kupewa stadi za karne ya 21 na kuziwezesha shule kupiga hatua   ziweze kufikia umahiri wa kutumia Tehama na kuwa shule za  dijitali.
3
MSEMAJI wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Dk Hassan Abbas amesema waandishi wa habari wanahaki ya kuikosoa serikali lakini hawapaswi kuandika habari za kuzusha na kupotosha.Amesema Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 kifungu cha 32 (2) kinatoa haki hiyo ya kila mwandishi kuikosoa serikali na kwamba kifungu cha 52 kinaeleza kwamba haitakuwa kosa kwa waandishi watakaoonesha makosa yaliyopo kwa serikali kwa uthibitisho na sio kuzusha.Hayo aliyasema jana jijini Dar es Salaam kwenye semina juu ya jukumu la wanahabari, iliyoandaliwa na Jumuiya ya Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mufti wa Tanzania na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwa niaba ya Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.Dk Abbas alisema kwa mara ya kwanza Tanzania imeweka kifungu hicho cha sheria ili kutoa haki ya kitaaluma kwa waandishi wa habari ambao ndio muhimili wa nne wa nchi, hivyo wanapaswa kutimiza wajibu wao katika jamii.Alisema mwandishi aliyefanya utafiti vizuri na kubaini madudu ndani ya serikali na akawa na vithibitisho vyote vyenye ukweli anauwezo wa kuandika habari na kuichapisha kwenye vyombo vya habari na sio kuandika habari za kizandiki."Tunapochukua hatua kali ya kulifungia gazeti kwa kuwa na habari zenye kuhatarisha usalama wa nchi au uzushi wanaharakati wengi wanalalamikia hatua hizo tunasahau kwamba waandishi pamoja na kuwa na haki wana wajibu wa kulinda nchi," alisema Dk Abbas.Aliongeza kuwa waandishi pia wana wajibu wa kuenzi na kulinda amani ya nchi kwa kukataa viashiria vinavyoharibu amani kwa sababu watu wa kwanza kuathirika ni wao wenyewe.Pia alisema kuwa katika mkataba wa Kimataifa wa haki za kisiasa na kiraia unaeleza haki na wajibu wa kitaaluma pamoja na mipaka yake. Alifafanua kuwa kama kutakuwa na habari za kupotosha ndani na nje ya nchi mkataba huo unaelekeza katika kanuni ya kukashifu au kumkejeri mtu, magazeti yatachukuliwa hatua kwa kufikishwa mahakamani."Ni kweli tunao uhuru wa kusema lakini ni wajibu wetu kutoandika habari za kukashifu mtu kwani ni kuvunja kanuni ya mkataba huu. Pia tunapaswa kuzingatia kanuni ya faragha tuandike habari lakini tuwe na ukomo ili kulinda faragha yake," alisisitiza.Dk Abbas alieleza kwamba ni vyema kuangalia usalama wa taifa kwa kuhakikisha kuwa yale mambo yanayohusiana na usalama siri zake zisitolewe kwa sababu zinaathiri ustawi wa nchi.Kwa mujibu wa Dk Abbas, sheria ya huduma za Habari inatoa haki ya kukusanya habari licha ya changamoto zilizopo, uhuru wa kuhariri na uhuru wa kusambaza taarifa hizo.Kwa upande wake, Kiongozi wa Waislamu dhehebu la Shia Ithnasheriya, Shekhe Hemed Jalala alisema wajibu wa mwandishi wa habari ni kuandika habari zenye kufuata misingi ya haki na sheria." Mwandishi wa habari mzalendo ni yule anayeitakia jamii isonge mbele kwa kuenzi mambo mazuri badala ya kuandika habari zinazofitinisha au kuhitilafiana au kuchochea jambo ambalo litaleta chuki baina ya jamii moja na nyingine" alisema Shekhe Jalala.Alibainisha kuwa mwandishi wa habari mzalendo ni lazima ataandika habari kuhusu rasilimali za nchi na maendeleo kwa jamii na kulinda amani, mshikamano na umoja. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake ( TAMWA) , Edda Sanga alisema bado vyombo habari havitoi fursa ipasavyo kwa waandishi wa habari wanawake hasa katika nafasi za juu za uongozi.Alisema vyombo vya habari vina uwezo wa kujenga na kubomoa hivyo vinapaswa kuona nafasi katika jamii kutafuta habari, kuhariri na kusambaza ili watu wengi wanufaike na kupata mabadiliko chanya."Mwaka 2008 ni wanawake watatu pekee ndio waliowahi kushinda kwenye Tuzo za Umahiri wa habari (EJAT) zinazotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT), ambao walishinda uandishi wa habari za uchunguzi," alisema Sanga.
3
Katika kipindi cha zaidi ya miongo mitano, mdada huyo amecheza zaidi ya filamu 150, zikiwemo zile kali kama Mr India, Chandni, ChaalBaaz na Sadma.Alikuwa akichukuliwa kama mmoja wa wanawake wachache wa Kihindi ambao wamepata mafanikio makubwa katika filamu bila kuwategemea mashujaa wakiume.Tangu akiwa na umri wa miaka minne, alikuwa akicheza filamu huko Tamil, Telugu, Malayalam, Kannada na Hindi.Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi alitwiti kuwa ameshtushwa na kifo hicho cha nyota huyo wa filamu nchini India, wakati Rais wa India, Ram Nath Kovind aliandika kuwa “Mshtuko”. Meya wa London, Sadiq Khan alitoa salamu za rambirambi kwa nyota huyo, akiandika katika Twitter:"Kwa kweli nilifurahia sana nilipokutana na nyota wa Bollywood Sri Devi wakati nilipotembelea India hivi karibuni."Ni huzuni kubwa kusikia taarifa za kifo cha msanii nyota kama huyo mwenye kipaji cha hali ya juu, katika uigizaji na utengenezaji wa filamu.”Msanii huyo alikuwa Umoja wa Falme za Kiarabu, ambako alikuwa akihudhuria sherehe za harusi za binamu yake, Mohit Marwah.Mume wa Sridevi, Boney Kapoor na mtoto wao wa kike, Khushi walikuwa pamoja naye wakati akiaga dunia Jumamosi, taarifa hizo zilisema. Shemeji yake, Sanjay Kapoor alisema kifo hicho kilitokea kama majira ya saa 5:00 usiku.
4
WAKATI michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ikiendelea kupamba moto, huku tukishuhudia mtifuano mkubwa wa mbio za marathon kwa mafahali wawili Simba na Yanga, kila mmoja wao akijinasibu kushinda michezo iliyobaki kuhakikisha anatwaa taji hilo msimu huu.Lakini vita nyingine ni kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam au FA, ambapo timu nne zinatarajiwa kuoneshana kazi zilizotinga hatua ya nusu fainali kwenye michuano hiyo, huku kila timu ikiwa na shauku ya kujihakikishia kukata tiketi kuiwakilisha nchi kwenye michuano ya kombe la shirikisho bara Afrika, Caf.Hadi sasa timu nne zimeingia kwenye hatua hiyo ambapo fainali ya kwanza timu kati ya Azam FC na KMC, ambayo ilitarajia kuchezwa jana wakati ile ya pili itazikutanisha Yanga dhidi ya Lipuli Mei 6.NUSU FAINALI YA KWANZAFainali hiyo ilitarajia kuwa ngumu na ilitarajiwa kupigwa jana jioni katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, ambapo wawili hao walikutana baada ya kufanya vyema kwenye michezo ya hatua ya robo fainali,ambapo KMC walipata fursa hiyo baada ya kuifunga timu ya African Lyon mabao 2-0 kwenye mchezo mgumu na wa kusisimua uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru.Huku Azam waliokuwa wa kwanza kutinga hatua hiyo baada ya kushinda mchezo wa ugenini kwa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar. mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.YANGA NA LIPULI FCMchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumatatu katika Uwanja wa Samora mjini Iringa, ambapo Lipuli inatarajiwa kuwa mwenyeji kumkaribisha bingwa wa kihistoria Yanga, mtanange huo unatarajiwa kuwa mgumu kutokana na uwezo wa timu zote mbili ulioneshwa kwenye michezo ya hivi karibuni kwenye michezo ya ligi. Kwa mara ya mwisho walipokutana katika uwanja huo katika mchezo wa Ligi Kuu mwenyeji Lipuli alifanikiwa kuibuka na pointi tatu baada ya kuifunga Yanga bao 1-0 mchezo uliotawaliwa na upinzani mkali mwanzo mwisho.Lakini safari hii mchezo huo unatarajiwa kuwa mgumu zaidi kwa kuwa hadi sasa Yanga bado ana wasiwasi ya kushindwa kutwaa ubingwa wa Ligi licha ya kuonekana hadi sasa anaongoza ligi hiyo kwa pointi 77 lakini bado mpinzani wake wa karibu Simba anashika nafasi ya pili kwa pointi 69 anaonekana kuja kwa kasi huku akiwa na faida ya michezo mitano mkononi ambazo kama atafanikiwa kushinda basi atafanikiwa kutetea ubingwa huo.Yanga walifanikiwa kutinga kwenye hatua hiyo baada ya kuifunga timu inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Namungo FC ya Lindi kwa mabao 1-0 mchezo ulipigwa kwenye Uwanja wa Majaliwa Lindi, huku Lipuli walifanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kuifunga Singida United kwa mabao 2-0.
3
Mechi kati ya Tanzanite dhidi ya Young She-Polopolo kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 20, itachezwa katika uwanja wa Azam Complex - Chamazi kuanzia saa 10:00 jioni.Kikosi cha timu ya Tanzanite chini ya kocha wake mkuu Rogasian Kaijage iliyoweka kambi eneo la Mbande na kufanya mazoezi yake katika uwanja wa Azam Complex kwa takribani wiki ya pili sasa kikijiandaa na mchezo huo.Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto, hali ya kambi ya Tanzanite ni nzuri wachezaji wote wapo katika hali nzuri na morali ya hali ya juu, kikubwa Watanzania wanaombwa kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi kuja kuwapa sapoti timu hiyo yataifa.Nayo timu ya Taifa ya U20 ya Zambia, Young She-polopolo inatarajiwa kuwasili leo Alhamisi jioni kwa ya Shirika la RwandAir, ambapo Ijumaa wanatarajiwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Azam Complex.Mwamuzi wa mchezo huo ni Batol Mahjob kutoka nchini Sudan, akisaidiwa na washika kibendera Remaz Osaman na Walaa Bilal, mwamuzi wa akiba Khadmallah Elasayed wote kutoka nchini Sudan na Kamisaa wa mchezo ni Flora Roosevelt kutoka nchini Malawi.Wakati huo huo, kikundi cha ushangiliaji cha timu za Taifa (Taifa Supporters) kimejiandaa kwenda kuwapa sapoti timu ya Tanzanite siku ya Jumamosi katika mchezo dhidi ya The Young She-Polopolo uwanja wa Azam Comlpex.Taifa Supporters baada ya kikao cha viongozi wao wamepanga kuwa na kikundi cha ushangiliaji cha watu wasiopungua 150 (mia moja hamsini) katika mechi hiyo ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 20.Wanachama wa kikundi cha Taifa Supporters watakutana Jumamosi saa 5:00 asubuhi kisha kuelekea uwanja wa Azam kwa ajili ya kuwashangilia Tanzanite katika mchezo huo.
4
KINSHASA, DRC              |               MAKAMU wa rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na mbabe wa kivita, Jean-Pierre Bemba, ameshindwa kupata vigezo ambavyo vingemwezesha kuwania urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Desemba 23, mwaka huu. Kwa mujibu wa majina ya awali yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya DRC, CENI, Bemba ni miongoni mwa wagombea sita wa urais waliokuwa wamewasilisha majina yao, lakini wameshindwa kujieleza kinagaubaga katika mahojiano ya saa kadhaa na tume hiyo. Juni mwaka huu, kiongozi huyo wa zamani wa waasi aliachiliwa huru baada ya mahakama kubatilisha hukumu dhidi yake ya uhalifu wa kivita. Tume ya Uchaguzi imesema Bemba amezuiwa kuwania kwa sababu alipatikana na hatia ya kuwahonga mashahidi katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC). Mwanasiasa huyo aliyerejea DR Congo mwanzoni mwa Agosti baada ya kukaa miaka 11 uhamishoni na gerezani, lakini alishinda rufaa yake ya kupinga hukumu aliyowasilisha katika ICC. Uchaguzi wa mwaka huu utafanikisha kuchaguliwa kwa mrithi wa Rais Joseph Kabila, ambaye muhula wake wa pili na wa mwisho wa kuongoza ulimalizika miaka miwili iliyopita. Muungano wa chama tawala nchini humo ulimteua waziri wa zamani wa mambo ya ndani, Emmanuel Ramazani Shadary kuwa mgombea wake. Kulikuwa na jumla ya watu 25 waliotaka kuwania nafasi ya urais, wakiwamo mawaziri wakuu wa zamani, Antoine Gizenga na Adolphe Muzito. Wawili hao pia wamekataliwa kuwania. Vyama vya upinzani vimelalamikia hatua hiyo ya Tume ya Uchaguzi hata kabla ya uamuzi huo kutangazwa rasmi, wakiituhumu serikali ya sasa kwa kujaribu kudhibiti na kuelekeza mchakato wa uchaguzi. Wagombea waliozuiwa kuwania, akiwamo Bemba, anayetazamwa na wengi kama mgombea atakayetoa ushindani mkali zaidi kwa muungano wa chama tawala, wanaweza kukata rufaa uamuzi huo wa kuondolewa majina yao. Orodha kamili na ya mwisho ya wagombea inatarajiwa kuchapishwa Septemba, mwaka huu. CENI imesema wagombea waliokidhi vigezo vya kuwania urais nchini humo ni kama ifuatavyo: Emmanuel Ramazani Shadary, Kikuni Masudi Seth, Mukona Kumbe Kumbe Pierre, Ngoy Ilunga Isidore, Makuta Joseph, Kabamba Noel, Mabaya Kinkiey Mulumba, Freddy Matungulu, Felix Tshisekedi, Allain Shekomba, Radjabu Sombolabo, Kamerhe Vital, Fayulu Martin Bomba, Gabriel Mokia, Basheke Sylvain, Charles Gamena na Mbemba Francis. Kiongozi mwingine wa upinzani, Moise Katumbi, anayemiliki klabu ya TP Mazembe, alizuiwa kurejea nchini DRC siku ya mwisho ya kuwasilisha nyaraka za kuomba kuwa mgombea wa urais.
2
Rubani Nelson Mabeyo, ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (CDF) Jenerali Venance Mabeyo ambaye alifariki jana, Jumatatu kwenye ajali ya ndege huko Serengeti, alikuwa mwajiriwa mpya wa Shirika la Ndege la Tanzania ATCL. Rubani Mabeyo na rubani mwanafunzi Nelson Orutu walipata ajali kwenye ndege ya kampuni ya Auric Air katika Uwanja wa Ndege wa Seronera na kufariki papo hapo. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi, rubani huyo alikuwa moja kati ya marubani 16 ambao walioajiriwa hivi karibuni na shirika hilo. Mhandisi Matindi aliongeza kuwa Nelson ilikuwa akahudhurie mafunzo maalumu ya kurusha ndege aina ya bombardier nchini Canada mara baada ya kuripoti kazini rasmi. “Captain Nelson Mabeyo alikuwa ni rubani bora aliyeshika nafasi ya pili, na ni moja kati ya marubani tuliokuwa tumewachukua kuwaajiri,” aliongeza. Matindi ameongeza kuwa Nelson alitakiwa kuondoka nchini kwenda Canada kwenye mafunzo hayo wiki iliyopita lakini alichelewa kwakuwa ilibidi amalizie mkataba wake na kampuni ya Auric.“Tumuombee, alikuwa kijana mdogo na mzuri,” aliongeza Matindi.
3
Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii (SSRA) imesema mabadiliko yaliyofanyika katika kanuni ya kikokotoo ya mafao ya uzeeni, yamelenga kumuongezea mstaafu mafao zaidi, kinyume na inavyodaiwa.Akizungumza na vyombo vya habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Dk Irene Isaka alisema mabadiliko ya kanuni kuhusu kikokotoo cha mafao ya uzeeni, yamemwongezea zaidi mafao mstaafu kuliko ilivyokuwa huko nyuma. Ni kwa bahati mbaya kwamba kumekuwa na baadhi ya wadau wameendeleza kampeni ya kupinga kanuni mpya ya kukokotoa mafao ya kustaafu, bila hata kuwa na taarifa sahihi na uelewa.“Fomula mpya ya kukokotoa mafao ya kustaafu na malipo ya pensheni imekuwa na tija zaidi kwa wachangiaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii kwa kuongeza kiwango cha mafao ya chini na kuongeza kiwango cha pensheni ya kila mwezi,” alisema Isaka.Alisema kupitia kanuni mpya ya kukokotoa malipo ya uzeeni, wachangiaji wa chini waliokuwa wanapata kati ya Sh 20,000 na Sh 50,000 kwa mwezi sasa watapata zaidi ya Sh 100,000 kwa mwezi.Alisema nadharia ya kwamba kuja kwa kikokotoo kipya, kunawaibia wachangiaji wa mifuko ya pensheni pindi wanapostaafu, siyo ya kweli kwa sababu sasa wachangiaji wanapata zaidi ya asilimia 117 ya michango yao waliyochangia wakiwa kazini. Dk Isaka alisema SSRA ni mamlaka inayosimamia zaidi matakwa na haki za wachangiaji kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii na kusema hawako tayari kuona fedha za wachangiaji zinaibiwa.“Kama kuna mtu yeyote anayependa ufafanuzi au kujua zaidi ni vizuri akawasiliana na SSRA kuliko kutoa taarifa za kupotosha kwa umma na kujenga hofu kwa wastaafu pasipo kuwa na msingi wowote,”alisema.Alisema mabadiliko mbalimbali yaliyofanyika katika sekta ya hifadhi ya Jamii, yalikuwa na lengo la kuhakikisha kwamba mwananchi au mwanachama, anayechangia katika mifuko ya hifadhi ya jamii wanafaidikia zaidi baada ya kustaafu.Dk Isaka alisema miongoni mwa maboresho yaliyofanywa kwenye sekta ya hifadhi ya jamii, ni kuongeza mikopo ya nyumba kwa wanachama, kuboresha mafao ya uzeeni kwa kuongeza pensheni ya kila mwezi na kuthaminishwa kwa pensheni ya mwezi.Maboresho mengine ni uanzishwaji wa fao la upotevu wa ajira, uanzishwaji wa fao la ugonjwa, kuweka kima cha chini cha mafao ya pensheni na kuboresha mafao ya warithi pindi mwanachama anapokufa.Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka hiyo, Onorius Njole alisema hatua zote muhimu mpaka kufikia hatua ya utekelezaji, zimeshirikisha wadau wote muhimu, likiwemo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) na wengin
3
KAULI ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaasha Tumbo kuwa Idara ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya hiyo haina mtendaji wa sekta ya ardhi anayeweza kuvaa viatu vya ukuu wa idara iwapo anayeshikilia nafasi hiyo, Salehe Kang’e ataondolewa, imemwokoa mkuu huyo wa idara kutumbuliwa.Kauli hiyo ilikuja baada ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angelina Mabula kueleza kuwa Mkuu wa Idara ya Ardhi katika halmashauri hiyo hafai kuwa mkuu wa idara ya ardhi kutokana na kushindwa kusimamia vyema ukusanyaji mapato yatokanayo na kodi ya ardhi.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Bakari Mhando alimwomba Anjelina kutomwondoa katika nafasi hiyo Kang’e, akidai upungufu aliouonesha atahakikisha unarekebishwa kwa mwezi mmoja.Akiwa katika ziara ya kustukiza katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga juzi, Dk Angelina Mabula alionesha kuchukizwa na mkuu huyo wa idara ya ardhi kushindwa kusimamia ukusanyaji kodi ya ardhi ikiwemo kutoa hati za madai kwa wadaiwa wa kodi ya ardhi wilayani humo.Kang’e amebakiza mwaka mmoja kustaafu kazi. Halmashauri hiyo imeingiza viwanja 3,000 katika mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi kwa njia ya kielektroniki na mashamba 1,009, lakini imetoa hati moja ya madai kwa wadaiwa wa kodi ya ardhi.Angelina alisema alichotegemea baada ya kuingizwa viwanja na mashamba kwenye mfumo huo wa ulipaji kodi kielektroniki, mkuu wa idara ya ardhi angehakikisha wadaiwa wote sugu wanafuatiliwa ili walipe kodi, lakini kinyume chake kazi hiyo haijafanyika na ni mdaiwa mmoja tu aliyepelekewa hati ya madai.Alisema msisitizo wa Serikali ni kukusanya mapato yakiwemo ya kodi ya ardhi ili kusaidia shughuli za maendeleo ambazo haziwezi kupatikana iwapo serikali haitakuwa na makusanyo mazuri ya kodi.“Haya yanayofanyika ununuzi wa ndege na ujenzi wa SGR (Reli ya Kisasa) bila ya kukusanya kodi hayawezi kufanyika na Rais John Magufuli anasisitiza ukusanyaji kodi, watu hawako makini,” alisema.Alimpa mwezi mmoja kuhakikisha wadaiwa wa kodi ya ardhi wanapelekewa hati za madai na watakaokaidi wafikishwe katika mabaraza ya ardhi na Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Kaskazini ifuatilie utekelezaji wa agizo hilo.
3
ZAIDI ya shule 300 za Serikali zilizopo vijijini zitapata kompyuta na kuunganishiwa mtandao intaneti kupitia programu ya pamoja kati ya Kampuni ya Vodacom na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF).Lengo la programu hiyo ni kuwezesha shule hizo kuunganishwa na mfumo wa kidigitali wa shule Tanzania, katika juhudi za kukuza elimu nchini. Tayari programu hiyo imeanza kunufaisha shule 10 mkoani Simiyu baada ya Vodacom kutoa kompyuta na kipanga njia (Router) zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 48 ikiwa kama sehemu ya mpango wake wa kusaidia ukuaji wa sekta ya elimu nchini.Akizungumza juzi wakati wa zoezi la utoaji wa vifaa hivyo kwa Shule ya Sekondari ya Simiyu iliyopo mkoani Simiyu, Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye alisema mchango wa kompyuta unaenda mbali katika kuunga mkono agizo la serikali la kukuza maendeleo ya kijamii vijijini na mijini Tanzania kupitia mfumo wa mawasiliano.“Vodacom imekuwa mshirika wa serikali katika maendeleo. Nina furahi kuona ushirika huu katika utekelezaji wa mradi wa serikali wa kuunganishwa kwa shule za umma nchini katika mfumo wa kidigitali. Tunashukuru sana kwa mchango huu na tunataka kampuni zingine kuiga zoezi hili katika kusaidia sekta ya elimu,” alisema Nditiye huku akieleza kuwa kufurahishwa na jitihada hizo zitakazonufaisha zaidi ya shule 300 zilizopo vijijini.Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Vodacom Foundation, Rosalynn Mworia alisema mpango huo ni sehemu ya ajenda ya kukuza mafunzo bora nchini Tanzania. Kompyuta hizo pia zitawezesha shule hizo kuunganishwa mfumo wa upatikanaji wa elimu kwa njia ya kidigitali kupitia mtandao wa Vodacom.Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa UCSAF Justina Mashiba alisema, “Tunajivunia kufanya kazi na Vodacom kuhakikisha mpango huu unafanikiwa kwa kuunganisha shule zote za umma na upatikanaji wa mtandao ili kutumia kikamilifu vifaa vya teknolojia ya habari na mawasiliano”. Hafla hiyo ilikuwa ni sehemu ya awamu ya kwanza ya michango ya kompyuta inayotolewa na Vodacom Foundation na UCSAF kwa shule za umma nchini.
3
MADRID, HISPANIA NYOTA wa Chelsea, Eden Hazard, anataka kuandika historia katika timu ya Real Madrid ya kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa kwa kiasi kikubwa cha fedha kuliko mchezaji mwingine katika historia ya timu hiyo. Wababe hao wa kihistoria wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, wanadaiwa kutenga kiasi cha pauni milioni 130, zaidi ya bilioni 378 za Kitanzania kwa ajili ya kumsajili kiungo huyo mshambuliaji raia wa nchini Ubelgiji. Hata hivyo, wamedai endapo watafanikiwa kumsajili mchezaji huyo, basi wataanza kumpa kiasi cha pauni milioni 88 zaidi ya bilioni 256 za Kitanzania, huku fedha zingine zikitarajiwa kutolewa kwa nyakati tofauti ikiwa pamoja na sehemu ya bonasi yake. Tayari uongozi wa timu hizo mbili umekutana kwa ajili ya kufikia makubaliano ya mwisho, hivyo siku za hivi karibuni Madrid watamtangaza mchezaji huyo ambaye ameonesha kiwango cha hali ya juu ndani ya Chelsea kwa kipindi cha miaka 7. Madrid haijawahi kufanya usajili wa bei kubwa kufikia hiyo ambayo wanataka kuifanya, kiasi kikubwa ambacho walikitumia kwa ajili ya kumsajili mchezaji na kuandika historia ni uhamisho wa Gareth Bale kutoka Tottenham na kujiunga na Real Madrid, Septemba 2013 kwa uhamisho wa pauni milioni 86, zaidi ya bilioni 250. Akifuatiwa na Cristiano Ronaldo ambaye alijiunga na Madrid akitokea Man United kwa uhamisho wa pauni milioni 80. Real Madrid wamekuwa wakiifuatilia saini ya Hazard tangu miaka miwili iliopita, hivyo kwa sasa dili hilo linaelekea ukingoni huku ikiwa tayari mchezaji huyo amewaaga wachezaji wenzake wa Chelsea pamoja na mashabiki baada ya kumalizika kwa mchezo wa Kombe la Europa dhidi ya Chelsea ambapo aliwasaidia kulitwaa taji hilo. Uhuamisho wa Hazard utakuwa mkubwa kwa wachezaji wa Ligi Kuu England, mchezaji ambaye anashikilia rekodi kwa sasa ni Philippe Coutinho, aliyejiunga na Barcelona miezi 18 iliopita akitokea Liverpool kwa uhamisho wa pauni milioni 145.
4
Na WAANDISHI WETU-DAR ES SALAAM/MWANZA RAIS Dk. John Magufuli ameagiza wafanyabiashara ndogo ndogo, maarufu machinga, wasibughudhiwe na wasiondolewe katika maeneo ya katikati ya miji wanayofanyia biashara kwani hakuna sheria inayowazuia. Rais Magufuli alimwagiza Waziri na Katibu Mkuu katika Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusitisha mara moja utekelezaji wa kuwaondoa wafanyabiashara hao. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais – Ikulu, Gerson Msigwa, Rais Magufuli akiwa na Makamu wake, Samia Suluhu Hassan, alitoa agizo hilo jana Ikulu na kuonya kuwa kiongozi yeyote ambaye hayupo tayari kulitekeleza aachie ngazi. “Kuna tabia wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi kufukuza wamachinga bila kufuata utaratibu, kama kuna asiyekubaliana na maagizo yangu, anaona yanamkwamisha, aache kazi hata leo. “Maagizo yamekuwa mengi, mengine yanakuwa na mwelekeo wa kuchonganisha Serikali na wananchi, nilizungumza hadharani sipendi wamachinga wafanye biashara kwenye hifadhi ya barabara, lakini hakuna sheria katika nchi hii inayosema mtu wa biashara ndogondogo au machinga hatakiwi kufanya biashara katikati ya miji. “Wamachinga wasibughudhiwe, hawakupenda kuwa machinga, naagiza Waziri na Katibu Mkuu katika Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusitisha mara moja kuwaondoa machinga katika Jiji la Mwanza pamoja na mikoa mingine mpaka hapo mamlaka husika zitakapokamilisha maandalizi ya maeneo watakapohamishiwa na kwa kuwashirikisha wamachinga wenyewe,” ilisema taarifa ya Ikulu ikimkariri Rais Magufuli. Aidha video iliyosambaa katika mitandao ya jamii jana, inamwonyesha Rais Magufuli akimweleza makamu wake umuhimu wa jambo hilo. “Nimeona nikuite wewe pamoja na hawa wa Tamisemi kwa ishu moja tu, unajua pamekuwa na maagizo mengi mengi, na maagizo mengine yanakuwa na mwelekeo wa kuchonganisha wananchi na Serikali, kwa bahati nzuri tuliozunguka kuomba kura kwa wananchi ni mimi na wewe pamoja na wabunge ndio wanajua shida halisi za wananchi. “Kwa hali inavyoelekea, pameanza kuwa panajitokeza amri za ajabu, hasa zinazotolewa na viongozi tuliowaamini kwamba watatekeleza yale tuliyowaambia. “Suala lililoniudhi ni hili suala la wamachinga… mimi na wewe tulizungumza kwamba tutatengeneza mazingira mazuri kwa watu hawa, watafutiwe maeneo ya kufanya biashara zao kwa utaratibu ulio mzuri. “Ishu iliyojitokeza Mwanza nawapongeza wamachinga hawakuleta fujo, nilizungumza kwenye mkutano wa Biafra hadharani, kwamba hawa wamachinga msiwatoe mjini na kama mnatengeneza mazingira mtengeneze mazuri ya kufanya biashara ili wasizagae. “Nilitoa mfano kwamba wanaweza kufunga barabara katikati ya mji, mkasema kwamba ndio sehemu yao kufanya biashara, lakini utaratibu umekuwa ondokeni mjini nenda Kiloleni… wanakoenda wala hawajawatengenezea mazingira mazuri, palikuwa na wanawake wanakaa Feri kuuza samaki, eti wanatolewa na kupelekwa sehemu gani, huko atauzaje samaki wake? “Wakitaka kuwahamisha wazungumze nao kwa utaratibu mzuri na wanakowapeleka liwe ni eneo rafiki kwao na watafaidika kufanya biashara, na polisi wanatumika vibaya, wanapaswa kuzungumza nao kwanza. “Ni lazima tujipange kutengeneza mazingira mazuri, tunapokuwa na wafanyakazi hewa zaidi ya 19,000, wanafunzi zaidi ya 65,000, mishahara hewa, hawapaswi kushangaa tunakuwa na wamachinga wengi katika nchi hii. “Tuliwatengeneza sisi, ni lazima tuwatengenezee mazingira mazuri ya kuishi, wawaache wamachinga wafanye biashara kwenye mazingira yao. “Nitoe wito kwa wamachinga, amri yangu hii isiwe chanzo cha wao kufanya biashara na kujenga mabanda kila mahali, hivyo basi wanapofanya biashara wasijenge mabanda kwa sababu yanachafua mandhari ya miji. WACHIMBAJI WADOGO Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameagiza Wizara ya Nishati na Madini kusitisha mara kuwaondoa wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Nyaligongo kilichopo katika Kata ya Mwakitolyo mkoani Shinyanga na badala yake waachwe waendelee na shughuli zao, na leseni ya mwekezaji anayedai eneo hilo ni lake aondolewe. “Wale waliofukuzwa Shinyanga wabaki palepale, kama ni leseni ya huyo mwekezaji ifutwe, Makamu wa Rais fuatilia hili, mweleze Waziri wa Nishati na Madini, waache kufukuza wananchi hovyohovyo, wale wanapata riziki yao, wanasomesha watoto wao, lakini wanafukuzwa tu. “Na hizi ndiyo ajira zenyewe, tulisema tunatengeneza ajira, wewe mwekezaji ni mmoja unakwenda kuwafukuza watu 5,000? Haiwezekani na wala haingii akilini,” alisisitiza Rais Magufuli. Pia alikemea vitendo vya wawekezaji wakubwa kupewa maeneo ambayo wachimbaji wadogo wanaendesha shughuli zao tena kwa mtindo wa kutengeneza nyaraka zinazonyesha mwekezaji husika alipewa eneo hilo kabla ya wachimbaji wadogo na kusisitiza kuwa mchezo huo hautavumiliwa. Alisema maagizo yake hayana maana kuwa wamachinga na wachimbaji wadogo waendeshe shughuli zao kwa kuvunja sheria bali wazingatie sheria na mamlaka zisiwanyanyase watu wanyonge.  MWANZA Tamko hilo la Rais Magufuli limeibua shangwe, vifijo na nderemo na kuwarejesha machinga waliokuwa wameondolewa katikati ya jiji la Mwanza na kubadili hali ya simanzi na huzuni iliyokuwa imetawala kwa muda wa siku tatu. Wafanyabiashara hao na mafundi magari waliondolewa kupitia operesheni iliyofanywa na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela kwa kuvunjiwa vibanda vyao vilivyokuwa katika maeneo ya mjini. Machinga hao walitakiwa kwenda katika maeneo ya Kiloleli, Nyegezi stendi, Buzuruga na mafundi wanaotengeneza magari  katikati ya mji walitakiwa kuhamia eneo la  Temeke-Mhandu na Sinai Mabatini. Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Mwanza, Said Tembo, alisema  anamshukuru Rais Magufuli kwa kusikiliza kilio chao kwa kuwa operesheni iliyokuwapo ilikuwa ya mateso, manyanyaso na maumivu makubwa kwa wanyonge. Agosti 13 mwaka huu, Rais Magufuli aliutaka uongozi wa Jiji na Manispaa za Dar es Salaam kutowaondoa wafanyabiashara ndogo ‘machinga’ katika maeneo waliyopo hadi watakapowatengenezea utaratibu mzuri wa kufanya biashara zao. Agosti 26 mwaka huu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene, alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuwaondoa wafanyabiashara hao maeneo ya Kariakoo kwa sababu wanaleta usumbufu na uchafu. HABARI HII IMEANDALIWA NA KULWA MZEE, JONNES RESPICHIUS (DAR ES SALAAM) NA JUDITH NYANGE (MWANZA)
3
Na ASHA BANI-DAR ES SALAM WAKALA wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) umewataka wananchi wanaofika katika ofisi ya wakala hiyo kupata huduma kuzingatia maelekezo yanayotolewa na viongozi na wataalamu wa afya kuhusu kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona. Kwa mujibu wa Meneja Masoko na Mawasiliano Rita, Josephat Kimaro alisema wakala umechukua hatua mbalimbali kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa huo lengo kubwa likiwa kuwalinda watumishi na wateja wanaofika kupata huduma katika ofisi zake kote nchini.  “Huduma zote za wakala zinaendelea kutolewa katika ofisi zetu kote nchini na kutokana kuhitajika na wananchi wengi kutokana na umuhimu wake katika maisha ya kila mmoja, hivyo imetubidi kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha tunayalinda makundi yote yanayohusika katika kutoa na kupata huduma,” alisema Kimaro. Alizitaja njia zinazotumika kupambana na maambukizi ya corona katika ofisi zote za wakala huo ni pamoja na kuweka maji, sabuni na vitakasa mikono katika milango yote ya kuingia katika majengo yao, kuhakikisha watumishi wote wa wakala wanavaa barakoa wakiwa kazini, kuweka vitakasa mikono katika maeneo mbalimbali ya ofisi na kuweka vifaa vya kuwapima joto kila mtu anayeingia katika jengo la Rita Makao Makuu.  Alisema maeneo yote ya ofisi kumewekwa matangazo yanayotoa maelekezo mbalimbali yanayohusiana na ugonjwa wa corona. “Pia wakala uliandaa mafunzo kuhusu ugonjwa wa corona iliyoendeshwa na mtaalamu kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini tunaendelea kuwasisitiza wananchi kuzingatia agizo la kuvaa barakoa wanapofika kupata huduma katika ofisi zetu na tunafurahi kuona asilimia kubwa  wanafuata maelekezo,” alisema Kimaro. Alisema pia wakala unaendelea kusisitiza wananchi kutumia njia mbadala za mawasiliano kupata huduma ambazo sio lazima kufika ofisi za wakala kama vile kupata maelezo kuhusu huduma zinazotolewa, kupakuwa fomu za maombi ya huduma zote, kuuliza maswali au kutoa maoni. Aliongeza kuwa wapo wananchi ambao wanafika ofisi za Rita kupata maelezo ya jinsi ya kupata cheti cha kuzaliwa na gharama zake au amepoteza cheti anawezaje kupata nakala wakati taarifa zote hizi zinaweza kupatikana bila yeye kufika ofisini. Alieleza njia mbadala za kupata taarifa hiyo ni pamoja na ukurasa wa facebook (facebook@ritatanzania) kupiga simu bure 0800 117 482, kutuma barua pepe info@rita.go.tz  na katika tovuti ya wakala www.rita.go.tz. 
3
Alisema hayo jana bungeni, alipokuwa akijibu hoja ya Mbunge wa Viti Maalumu, Susan Lyimo (Chadema), aliyedai katika swali lake la nyongeza kuwa, fedha hizo zinatolewa kwa kufuata itikadi za chama.Akifafanua jibu hilo, Chiza alisema mifuko ni mingi na mingineiko katika sekta, na suala muhimu ni kwa wajasiriamali kufahamu kwanza mifuko hiyo na maeneo ilipo.Chiza alisisitiza kuwa itikadi ya chama si masharti ya kupata mikopo, kwa kuwa walengwa ni Watanzania wote wa kipato cha chini na hata agizo la Rais Jakaya Kikwete, lilitaka wanufaika wawe wajasiriamali wadogo.Kuhusu utendaji wa mifuko hiyo, Chiza alisema Serikali inafanya tathmini ya waliopata mikopo na karudisha kwa kuwa mikopo hiyo itakuwa endelevu pale tu waliopatiwa watakapoirudisha kwa wakati, ili wengine nao wapate.Awali katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalumu, Josephine Genzabuke (CCM), alisema mfuko wa wajasiriamali wadogo, maarufu ‘Mabilioni ya JK’ umevutia vijana wengi lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwamagumu.Genzabuke pia alitaka Serikali ieleze ina mkakati gani wa kuhakikisha mfuko huo unakuwa endelevu kwa lengo la kunufaisha wanyonge.Akitoa majibu ya hoja hiyo, Chiza alisema lengo la mfuko huoni kuwezesha wananchi wa mijini na vijijini kupata mikopo na kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato.Alisema masharti ya kupata mkopo huo si magumu ikilinganishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hiyo ni asilimia 10, ikilinganishwa na ile inayotolewa na mabenki ambayo ni zaidi ya asilimia 20.Mbali na riba ndogo, Chiza alisema pia wananchi ambao wanapata mikopo hiyo, hawahitaji kuwa na dhamana kama ilivyo katika mabenki.Katika kuhakikisha inakuwa endelevu, Chiza alisema tathimini itakayofanyika italenga kubaini vikundi na wajasiriamali walionufaika, shughuli wanazozifanya, maendeleo ya shughuli hizo na changamoto zilizojitokeza.Alisema matokeo ya tathimini hiyo itakayofanyika mwakani, yataiwezesha Serikali kuendeleza mfuko huo kwa njia bora zaidi, ikiwemo kuandaa utaratibu mzuri zaidi wa mikopo hiyo.
5
Akitoa mada kwenye mkutano unaohusu matumizi ya sayansi na teknolojia katika kukuza uchumi wa nchi jana jijini Dar es Salaam, Mhadhari wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Juma Kitima alisema vivutio hivyo vinaweza kuwa hasi au chanya.Alisema maji yanayotumika viwandani yakichujwa yanaweza kuhifadhiwa na yakatumiwa tena kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji, uzalishaji wa umeme na matumizi mengine ya manufaa kwa maisha ya binadamu.Alisema miongoni mwa vivutio hivyo ni kuwasamehe ushuru wenye viwanda mara wanapoagiza mitambo hiyo ambayo alikiri kuwa gharama za ujenzi wa mitambo hiyo ni mkubwa.Alitoa mfano kuwa walifanya utafiti na wakashirikiana na kiwanda cha pombe kali cha Banana kilichoko mjini Arusha kujenga mtambo huo ambao uligharimu Sh milioni 800.Hata hivyo alisema mtambo huo ni bora zaidi na una faida kubwa kwa mwenye kiwanda na jamii inayokizunguka kiwanda hicho.Lakini pia alisema Serikali inaweza kutunga sheria kali zitakazowabana wenye viwanda na akasema kwa sasa wenye viwanda wanaendelea kuharibu mazingira kwa vile hakuna sheria inayowabana na hata kama ipo haiheshimiwi.Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Dk Hassan Mshinda alisema mkutano huo ulikuwa unajadili mambo kadhaa kuhusu mradi ulionzishwa kati ya tume hiyo na Shirika la Maendeleo la Sweden kuona namna ambavyo sayansi inaweza kusaidia kukuza uchumi na utunzaji wa mazingira.Alisema mkutano huo pia ulikuwa na lengo la kuona namna ambavyo Serikali inaweza kushirikiana na sekta binafsi katika kufadhili tafiti mbalimbali kwa manufaa ya jamii na akatoa mfano kuwa utafiti wa Profesa Kitima kwenye kiwanda cha Banana ni mfano wa mashirikiano hayo.Naye Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha Banana Investiment cha mjini Arusha Adolf Olomi, alisema kabla ya kujenga mtambo huo, kulikuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuwa kiwanda hicho kilikuwa kinachafua mazingira, lakini kwa sasa mambo ni shwari.Alisema maji yanayotoka kiwandani yanachujwa tena na mtambo huo na wanayatumia kwa ajili ya umwagiliaji na wanaangalia namna ambavyo wanaweza kutumia maji hayo kuzalisha umeme utakaotumiwa na kiwanda hicho.
5
Na Ester Mbussi – Dodoma SERIKALI imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma wa mwaka 2017, ambao una takribani mapendekezo 17 yanayouma na kupuliza. Mapendekezo hayo, ni pamoja na kuunganisha mifuko ya LAPF, PPF, GEPF na PSPF na kuanzisha mfuko mmoja kwa watumishi wa umma na kufuta sheria zilizoanzisha mifuko hiyo. Mswada huo pia unapendekeza utoaji wa mafao manane ambayo ni fao la pensheni, warithi, ulemavu, uzazi, ukosefu wa ajira, ugonjwa na fao la kufiwa. Pia unapendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), ili kuufanya mfuko huo kuwahudumia wafanyakazi sekta binafsi. Kwa mujibu wa muswada huo uliowasilishwa bungeni jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, mswada huo unapendekeza kuanzishwa kwa fao la upotevu wa ajira (Unemployment Benefit), ili kuondoa changamoto ya muda mrefu ya wanachama kujitoa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Alisema watakaonufaika na fao hilo ni wanachama ambao hawajafikisha umri wa miaka 55. “Aidha, mwanachama atakayenufaika na fao hilo pia ni yule ambaye hajaacha kazi kwa matakwa yake, awe Mtanzania, awe amechangia kwa kipindi kisichopungua miezi 18 na ametoa uthibitisho kwa mkurugenzi kuwa hajaweza kupata kazi nyingine. “Aidha, mfuko utamlipa mwanachama aliyekidhi vigezo mafao yake hata kama mwajiri hajawasilisha michango na baadaye mfuko utafuatilia michango ambayo haijawasilishwa kutoka kwa mwajiri,” alisema. Kipengele hicho cha fao la upotevu wa ajira, kilizua mjadala baada ya baadhi ya wabunge kudai ni fao la kujitoa limeletwa kivingine. Mhagama alisema mswada huo pia unapendekeza kuboresha masharti kuhusu fao la uzazi ambapo licha ya kupata fedha taslimu baada ya kujifungua, mwanachama pia atapata huduma ya matibabu kabla na baada ya kujifungua endapo huduma hizo hazilipwi na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Mhagama alisema fao hilo litatolewa mara nne kwa mwanachama katika kipindi chake chote cha ajira. “Sheria hii inalenga kuimarisha mfumo wa usimamizi na udhibiti wa sekta ili kuwezesha Mamlaka ya Hifadhi ya Jamii (SRRA) kuendelea kusimamia sekta hiyo ili kuhakikisha mabadiliko hayaathiri kwa namna yoyote masilahi ya wanachama wastaafu,” alisema Mhagama. Alisema muswada huo ukipita na kuwa sheria, wanachama wa mifuko hiyo watajipatia mikopo ya nyumba na shughuli nyingine za kiuchumi kwa riba nafuu. Mhagama alisema lengo la kuunganisha mifuko hiyo ni kuondoa uwepo wa mifuko mingi ya pensheni inayotoa mafao yanayofanana na kupunguza gharama za uendeshaji. Alisema hatua hiyo pia itapunguza gharama za uendeshaji kutoa viwango vya asilimia 19 hadi asilimia tisa iliyowekwa na mdhibiti, kupunguza migogoro baina ya mifuko, kuboresha mafao ya wanachama na kuongeza tija katika sekta ya hifadhi ya jamii. “Sheria inaweka utaratibu bora na rahisi wa wanachama wa mifuko iliyounganishwa kuhamia kwenye mfuko mpya bila kuathiri mafao yao na uendelevu wa mifuko mipya na wanachama waliopo katika sekta binafsi, ambao kwa sasa wanaochangia kwenye mifuko hawatahamishwa na badala yake utaratibu mpya wa mifuko miwili utaanza kwa wanachama watakaoajiriwa baada ya sheria. “Pia hiyo imeweka bayana kuwa mafao na michango ya wanachama haitatozwa kodi kama ilivyokwishabainishwa katika sheria za kodi na viwango vya uchangiaji na namna ya uchangiaji katika mfuko, ambapo kiwango cha uchangiaji kitakuwa asilimia 20 huku mwajiri atachangia asilimia 15 na mwajiriwa akichangia asilimia tano ya mshahara,” alisema. KAMBI RASMI YA UPINZANI Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Msemaji wa Kambi hiyo, Esther Bulaya, alisema wanashauri kuanzishwa kwa mchakato wa kuifuta SSRA kwani kuendelea kuwepo kunaongeza gharama zisizokuwa za lazima. “Kifungu cha 24 cha muswada kinatoa ruhusa kwa mwanachama kujitoa kwa sharti la kupata kibali cha bodi na kisha bodi kujiridhisha kuwa mwanachama amekidhi matakwa yaliyowekwa. “Umuhimu wa fao la kujitoa kama sheria ya PPF na PSPF zilizvyokuwa zinahitaji, tukumbuke kuwa kanuni zinaletwa na SSRA kujaribu kuzuia fao la kujitoa ambalo lilileta mtafaruku kwa wanachama, hasa wale waliokuwa wameajiriwa katika sekta ya madini. “Aidha, vifungu vya 66 na 67 vya muswada vinatoa uhuru kwa Mkurugenzi Mkuu wa PSPF kuomba kibali cha mahakama ili kukamata mali za mwajiri, lakini akashindwa kulipa wakati kifungu cha 72 kinazuia mali za mfuko kukamatwa na kunadiwa bila kuwepo kibali cha waziri, Kambi Rasmi inauliza, kwanini mali zake zisikamatwe kama kutakuwa na amri ya kufanya hivyo, hii tunaona ni ‘double standard’ inayowekwa katika muswada huu,” alisema Bulaya.   MAONI YA KAMATI Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba, alisema kuunganishwa kwa mifuko hiyo kutapunguza gharama za uendeshaji. Alisema mwaka 2014/15 LAPF pekee ilitumia Sh bilioni 1.8 wakati GEPF ikitumia Sh milioni 300, tofauti ya Sh bilioni 1.5 sawa na asilimia 83.3 kwa gharama za uendeshaji wa bodi ya wadhamini. Serukamba pia alisema kamati yake inashauri Serikali iongeze aina mbili za mafao kutoka nane yanayotolewa na mfuko hadi 10 kwa kuongeza fao la elimu na fao la mkono wa kwaheri (gratuity benefit).   MICHANGO YA WABUNGE Akichangia maoni kuhusu muswada huo, Mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Masele, alisema kutokana na kuondoa fao la matibabu ambalo lilikuwa likitolewa na mifuko mingine, ni vyema Serikali ikaangalia utaratibu wa kuwawezesha watumishi kupata huduma hiyo kupitia Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF). Alisema Watanzania wengi wako katika sekta isiyo rasmi na wengi hawaratibiwi na mfuko wowote, kwahiyo uamuzi huu unawafanya wengi waratibiwe na utawanufaisha wengi. “Napendekeza Serikali ilete marekebisho, iongeze fao la bima ya afya ili wanachama watakaochangia katika mfuko mpya utakaoanzishwa katika fao hili waweze kuchangia tena NHIF. “Mwenyekiti ukitazama kwa makini utaona watumishi wa umma watakuwa wanachangia mara mbili, wanakatwa NHIF ili wachangie huduma, lakini pia wanakatwa huku kwenye mfuko, sasa fedha hizo zielekezwe NHIF kwa wanachama wapya ili kuwaondolea kuchangia mara mbili,” alisema. Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, alisema mfumo wa nchi unahusisha watu ambao wameajiriwa katika sekta rasmi tu, kwahiyo kuna haja ya kuangalia utekelezaji wa kisera na kisheria katika hifadhi za jamii ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi. “Leo hii korosho ina bei nzuri sana na wananchi wamepata fedha nyingi, lakini kesho bei ya soko la dunia ikiporomoka watu watalia kwa sababu hatuna mfumo wa hifadhi ya jamii kwa wakulima ambao tungeweza kuwapa fao la bei pale ambapo bei zitakuwa zimetetereka. “Sasa hivi NSSF ina watu 600,000, Serikali inaenda kutunga sheria kuwaondoa watu 600,000 kwenye takwa la kisheria la bima ya afya, naelewa mkanganyiko ambao Serikali inaupata kwamba inataka bima za afya zote ziunganishwe NHIF. “Inaeleweka tunachopaswa kusema kwamba fao hilo litatolewa na NHIF kwa hiyo NSSF ichukue ile michango ambayo imetolewa na wanachama kwamba asilimia ngapi ya michango inalipia bima ya afya ipelekwe huko na ukiwa na kadi ya NSSF basi moja kwa moja unakuwa mwanachama wa NHIF,” alisema Zitto. Naye Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago (Chadema), alisema ukokotoaji wa mafao lazima uwekwe kwenye sheria na si uingizwe kwenye kanuni zitakazotungwa na waziri. Alisema ukokotoaji ukiwekwa wazi kwenye sheria utamwezesha mfanyakazi kufahamu kiwango halisi cha mafao atakachokipata pindi akistaafu. Pia alisema kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kusiweke kando faida muhimu zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya mifuko hiyo, hususani fao la matibabu na elimu.
3
Na LEONARD MANG’OHA-DAR ES SALAAM MOTO unaodaiwa kusababishwa na kutoboka   bomba la gesi umeteketeza baadhi ya nyumba na vibanda katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani,  Dar es Salaam. Taarifa za   tukio hilo zilianza kuenea katika mitandao ya jamii saa 11:00 na kuzua taharuki kwa wananchi. Iilielezwa kuwa  nyumba zaidi ya tatu ziliwaka moto katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani  kutokana na moto huo wa bomba la kusafirisha gesi lililopasuliwa. Mashuhuda waliiambia MTANZANIA kuwa mafundi wa Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam( Dawasco) walikuwa wanabadilisha mabomba ya maji ndipo walipolipasua bomba hilo la gesi linalopita katika eneo hilo. Kupasuka kwa bomba hilo kulisababisha watu kukimbia huku na kule ili kuuona huku wengine ikiwa ni njia ya kujinusuru. Hali hiyo ilisababisha barabara ya Buguruni kwa Mnyamani kwenda Vingunguti kufungwa huku treni inayofanya safari kati ya Stesheni na Ubungo ikisimamisha safari kutokana na moto huo. Akizungumzia hali hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kapuulya Msomba alisema  bomba hilo lilipasuliwa na wafanyakazi wa Dawasco. “Tunashuru zimamoto wameshafika hapa hivyo hakuna tabu, tunaimani watauzima moto huo. “Ninachowaomba wananchi wasikimbilie eneo lenye hatari, wawaachie Kikosi cha Zimamoto wafanye kazi yao,’’ alisema Msomba.
3
LONDON, ENGLAND KIUNGO mpya wa klabu ya Liverpool, Alex Oxlade-Chamberlain, amedai maamuzi yake ya kuondoka katika klabu ya Arsenal na kujiunga na kikosi cha kocha Jurgen Klopp, yalikuwa magumu kwake, lakini hawezi kuwaomba radhi mashabiki kuondoka kwake. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24, alijiunga na kikosi cha Arsenal tangu mwaka 2011, kabla ya kujiunga na Liverpool katika kipindi hiki cha majira ya joto dakika chache kabla ya kufungwa kwa usajili. Mchezaji huyo amejiunga na Liverpool kwa kitita cha pauni milioni 35, baada ya kukataa ofa kwa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu nchini England, Chelsea, lakini amedai Arsenal ni sehemu ya maisha yake, hivyo kufanya maamuzi ya kuondoka, jambo ambalo lilikuwa gumu kwake. Katika kipindi cha miaka sita aliyokaa ndani ya kikosi hicho cha Arsenal alifanikiwa kushinda taji la Kombe la FA mara tatu. “Kuondoka Arsenal yalikuwa maamuzi magumu sana katika maisha yangu, kwanza napenda niwashukuru mashabiki wa klabu hiyo ya Arsenal kwa sapoti yao waliyonipa katika kipindi changu chote, lakini siwezi kuomba radhi maamuzi yangu ya kuondoka. “Niliamua kufanya hivyo kwa ajili ya kufungua ukurasa wangu mpya wa maisha ya soka, sikutaka kuondoka huku nikiwa na mgogoro na timu, nadhani ulikuwa wakati wangu sahihi wa kufanya hivyo. “Wakati nipo Arsenal nilikuwa namwangalia kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp kila anachokifanya kwa wachezaji wake, hivyo nilivutiwa kwa kiasi kikubwa na nilitamani kuwa mmoja wa wachezaji wake. “Klopp ni mmoja wa makocha ambao wanaweza kukushawishi, kukujenga, hivyo nikaona bora niondoke Arsenal ili niyapate hayo kwa Klopp, ninaamini hapa nilipo nitafanikiwa kwa hilo, kutokana na uwezo wa kocha pamoja na umoja wa wachezaji, kutokana na hali hiyo naweza kuja kuwa mmoja wa wachezaji wenye uwezo mkubwa duniani,” alisema Chamberlain. Mchezaji huyo katika klabu ya Arsenal alifanikiwa kucheza jumla ya michezo 132 ya Ligi Kuu tangu ajiunge mwaka 2011 na kufanikiwa kufunga mabao tisa, wakati huo kabla ya kujiunga na Arsenal alikuwa anakipiga katika kikosi cha Southampton, huko alicheza michezo 36 ya Ligi na kufunga mabao tisa.
4
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imesema ipo tayari kupitisha fedha kwa ajili ya kuendeleza Mradi wa Kuwezesha Umilikishaji Ardhi (LTSP) katika mikoa yote nchini, baada ya kuridhishwa na majaribio ya mradi huo kwenye wilaya tatu za Kilombero, Malinyi na Ulanga mkoani Morogoro.Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Nape Nnauye alisema hayo hivi karibuni wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mbuga, kilichopo wilayani Ulanga mkoani Morogoro.Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake, ilipata fursa kutembelea wilaya za Ulanga na Kilombero kwa lengo la kukagua utekelezwaji wa Programu ya kuwezesha Umilikishaji Ardhi (Land Tenure Support Programme - LTSP) unaotekelezwa wilaya tatu za Ulanga Kilombero na Malinyi.Mwenyekiti huyo alisema, kutokana na muitikio mkubwa wa wananchi wa kujitokeza kupimiwa vipande vyao vya ardhi katika vijiji vya wilaya hizo tatu ni muhimu kwa mradi huo sasa ukaendelezwa kote nchini.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , William Lukuvi aliyeambatana na kamati hiyo, aliwataka wasimamizi na watekelezaji wa mradi kuweka usawa wa kijinsi katika kufanikisha mradi huo ili wanawake nao wanufaike na ardhi.Mkuu wa Wilaya ya Ulanga, Ngollo Malenya aliuomba uongozi wa mradi huo kuongeza muda ili kukamilisha kwa baadhi ya vijiji ambavyo upimaji wake wa ardhi ulikuwa bado haujamalizika licha ya majaribio hayo kufikia ukingoni.Meneja wa mradi huo , Godfrey Machabe amesema lengo la mradi huo ni kupunguza ama kuondosha kabisa migogoro ya ardhi kwa kupima na kutoa hati za hakimiliki za kimila.Awali, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kabla ya kufanya ziara katika wilaya hizo ilipewa taarifa ya mkoa na Katibu Tawala wa mkoa huo, Clifford Tandari,ambayo ilionesha jumla ya mipaka ya vijiji 127 imepimwa.Licha ya mipaka ya vijiji hivyo pia jumla ya vipande vya ardhi 263,028 vimehakikiwa na kupimwa ikiwemo na migogoro mikubwa ya ardhi 58 ya mipaka ya vijiji imetatuliwa.
3
WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kuhitimisha Ligi ya soka la Watu wenye ulemavu itakayofanyika leo katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Dar es Salaam.Pamoja na Dk Mwakyembe pia atakuwepo Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera, Ajira na Wenye Ulemavu Stella Ikupa, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, Meya wa manispaa ya Ilala, Omar Kumbilamoto na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu la Dunia (WAFF), Simon Baker.Akizungumza jana Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka la watu wenye ulemavu Tanzania (TAFF), Moses Mabula alisema zitachezwa michezo miwili ambayo itazikutanisha Drogheda AFC na River Valley na mchezo mwingine ambao utaamua nani bingwa utakuwa kati ya Bullymum AFC na L.S.L AFC.“L.S.L AFC inaongoza ikiwa na pointi tisa baada ya kucheza michezo minne na kufungwa mmoja ikifuatiwa na Ballymun hivyo timu itakayoshinda itakuwa bingwa,” alisema Moses. Pia alisema sherehe za kufunga ligi hiyo zitaanza saa 8:00 mchana na kuwaomba mashabiki kufika kwa wingi kwani hakuna kiingilio.Alisema bingwa atapata kombe na medali na wachezaji waliofanya vizuri nao watapata medali na wengine watachaguliwa kuunda timu ya Taifa ambayo inatarajiwa kushiriki mashindano ya CECAFA mwakani na baadae mashindano ya Afrika yanayotarajiwa kufanyika Septemba mwakani nchini Angola.Katika msimamo wa wafungaji mchezaji wa Drogheda AFC , Winston Alex anaongoza akiwa na mabao sita akifuatiwa na Alfan Kiyanga wa L.S.L, Juma Kidevu wa Ballymun na Saleh Yusuph wa River Vallaey ambao kila mmoja ana mabao matano.Frank Ngairo wa L.S.L ana mabao manne, Modrick Mohamed wa Drogheda ana mabao matatu, Salim Rashid na Steven Manumbu wote wa Ballymun wana mabao mawili kila mmoja na Athuman Lubandame na Salmin Michael wa L.S.L wana bao moja kila mmoja. Tanzania tayari ni mwanachama wa Shirikisho la Soka la Watu wenye ulemavu la dunia.
4
SAKATA la tishio la mgomo wa madereva wa mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani umetinga bungeni ambapo serikali imeombwa kukaa na wafanyabiashara wa vyombo vya usafi ri ili kutafuta suluhu ya tozo na adhabu mbalimbali zinazolalamikiwa. Suala hilo lilitinga bungeni jana baada ya Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM) kuomba bunge lisitishe shughuli zake na kujadili suala hilo akidai ni la dharura.Aliomba Bunge kuahirisha kazi zake zilizopangwa jana na kujadili tishio la mgomo wa madereva wa mabasi hayo akisema baadhi yameanza kusitisha utoaji wa huduma ya usafiri. Alitoa mfano wa adha hizo kuwa ni kufungwa kwa Vifaa Maalumu vya Kudhibiti Mwendokasi wa Basi (VTS) ambavyo vinaangaliwa na maofisa wa Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kutoka mabasi yanapoanzia safari hadi yanapomaliza na dereva akibainika kuongeza mwendo anapewa alama moja. Alisema mbali ya vidhibiti mwendo pia zipo alama za barabarani nyingi akatoa mfano kuwa umbali wa Dar es Salaam na Chalinze ambao ni kilomita 193 kuna vibao vya kupunguza mwendo zaidi ya 93 na mabasi hayo yanatakiwa kwenda umbali wa kilometa 50 kwa saa na kuwa ukijumlisha na matuta ya barabarani, dereva anaweza kutumia saa sita. Alisema dereva asiposimama kwenye eneo la wapita kwa miguu au kwenye eneo linaloonesha pungufu ya kilometa 80 kwa saa anapewa alama, na katika barabara hiyo anaweza kujikuta anapewa alama nyingi kwa siku moja. Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson akijibu mwongozo huo, alisema jambo hilo si la dharura kwa Kanuni za Bunge Kifungu cha 47 (4) na 48 (4) kwani halikutokea mapema katika siku hiyo.Alisema lakini kutokana na umuhimu wa jambo hilo, serikali inatakiwa kuchukua hatua ili kuhakikisha inakaa na wamiliki na madereva wa mabasi hayo ili kujadiliana kwa kina suala hilo kwa kuangalia namna bora ya kuondoa kero zilizopo lakini pia kulinda maisha ya watu. Dk Tulia alisema vitendo hivyo vinavyofanywa kwa madereva ni uonevu kwani katika kufikia uchumi wa kati watu wanatakiwa kusafiri kwa haraka kutoka eneo moja hadi nyingine kwa shughuli za uzalishaji, lakini wakizingatia usalama wa safari zao. Mwanzoni mwa wiki kulikuwa na hoja ya kuanza kwa mgomo kwa madereva wa magari yaendayo mikoani kutokana na kutozwa gharama mbalimbali ambazo zinazidi uendeshaji wa shughuli zao lakini hata hivyo juzi Sumatra ilikanusha taarifa za kuwepo kwa mgomo huo.
3
WIZARA ya Maji imewasilisha makisio ya bajeti ya wizara hiyo, ambayo ni zaidi ya Sh bilioni 634.196. Fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ni Sh bilioni 610.469, zitakazotumika kukamilisha miradi mbalimbali ya maji nchini.Aidha, upatikanaji wa maji katika maeneo ya vijijini, umeongezeka mwaka mmoja uliopita kutoka asilimia 58.7 hadi asilimia 64.8 huku wa mijini ikifika asilimia 80 Akisoma hotuba ya Bajeti ya mwaka 2019/20, Waziri wa Maji, Profesa Mbarawa alisema kiasi hicho cha fedha, kimelenga kufikisha majisafi na salama kwa asilimia 85 kwa vijijini na asilimia 90 kwa mjini ifikapo mwaka 2020.Kati ya fedha zilizoombwa, zaidi ya Sh bilioni 23.7 zitatumika kwa ajili ya matumizi ya kawaida na fedha za mshahara kwa wafanyakazi za wizara na chuo cha maji. “Kati ya fedha za maendeleo Sh bilioni 610.469 za maendeleo, Sh bilioni 349.449 sawa na asilimia 57 ni fedha za ndani na Sh bilioni 261.020 sawa na asilimia 43 ni fedha za nje,” alisema.Katiba hotuba yake, Mbarawa alisema miradi inayotarajiwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha ni pamoja na utafutaji wa vyanzo vipya vya maji. Aidha, serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Oman, itachimba visima 100 kwa ajili ya kusambaza maji katika shule za sekondari na msingi.Katika kufikia azma hiyo, maeneo 98 katika shule za msingi 58 na sekondari 40 yalifanyiwa utafiti kwa ajili ya kuchimba visima. Pia serikali itatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya uondoaji majitaka kwa kushirikiana na Serikali ya Korea Kusini, utakaogharimu dola za Marekani milioni 90.Alisema hadi Aprili mwaka huu, mtaalamu mshauri atakayesimamia mradi huo amepatikana na ameanza kazi ya mapitio ya usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni “Mradi huu utahusisha ujenzi wa mfumo wa majitaka wa mabomba yenye urefu wa kilometa 376 kutoka maeneo ya katikati ya jiji, Ubungo, Kinondoni, Mwananyamala, Msasani na Ilala hadi kwenye mtambo wa kusafisha majitaka utakaojengwa eneo la Jangwani,” alieleza.Alisema kuwa mtambo utakuwa na uwezo wa kusafisha lita milioni 200 za maji taka kwa siku. Vilevile alisema ujenzi wa mradi huo, utahusisha kubadili mwelekeo wa bomba linalomwaga majitaka baharini na kuyapeleka kwenye mtambo wa Jangwani.“Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza katikati ya mwaka 2019/20 na serikali imetenga Sh bilioni 10 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Profesa Mbarawa alisema hadi kufikia Aprili mwaka huu jumla ya miradi ya maji 1,659 yenye vituo vya maji 131,370 imejengwa. Kati ya vituo vilivyojengwa, vituo 86,780 vinafanya kazi na uwezo wa kuwahudumia watu watu 25,359,290 ambao ni sawa na asilimia 64.8 ya wananchi waishio vijijini.Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mahmoud Mgimwa aliomba serikali kuongeza tozo kutoka Sh 50 hadi Sh 100 kutoka kwenye mafuta au chanzo kingine kwa ajili ya kuongeza fedha zitakazogharamia miradi ya maji kupitia Mfuko wa Taifa wa Maji.“Kwa miaka mitatu sasa kamati imekuwa ikiishauri serikali kuimarisha makusanyo ya Mfuko wa Taifa wa Maji kwa kuongeza tozo ya mafuta kwa kila lita ya petroli na diseli kutoka shilingi 50 hadi shilingi 100. Kutotekelezwa kwa ushauri huo kunaathiri ufanisi wa utekelezaji wa miradi ya maji hususan kwa maeneo ya vijijini” alisema.
3
Tunu Nassor na Christina Gauluhuanga, Dar es salaam MWILI wa Mwandishi wa Habari Eliya Mbonea, umeagwa jana Hospitali ya Taifa Muhimbili na unatarajiwa kuzikwa leo jijini Arusha huku mtu wa mwisho kuwa naye wodini akieleza kauli yake ya mwisho kabla ya kukata roho. Mbonea hadi anafikwa na umauti alikuwa akiandikia magazeti ya Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, akiwa mwakilishi wake kwenye mikoa ya Kanda ya Kaskazini. Mchungaji wa Kanisa la Anglikana, Joseph Opio jana alisema wameshindwa kufanya ibada ya kuaga mwili wa marehemu kwa sababu Serikali imezuia ibada hizo kwa sababu zinakutanisha watu wengi wakati huu wa janga la corona. Akizungumza na MTANZANIA, Mchungaji Opio alisema amepatwa na mshtuko kutokana na kifo cha Mbonea. Alisema siku ya kifo chake alikuwa naye wodini ambapo alikuwa akijiandaa kupata ruhusa ya kutoka na muda mfupi akaletewa matunda akaomba aingie chooni kwanza. Alisema cha kushangaza baada ya kutoka chooni akasema anajisikia vibaya kwakuwa ametapika alivyoingia chooni. “Tulishangaa kwa dakika chache akajilaza kitandani na kuanza kulalamika anaishiwa hewa na wakaja madaktari wakajaribu kumwongezea oksijeni, lakini ikashindikana na ndio ikawa mwisho wa Mbonea. “Inauma sana, baada ya hali hiyo alimwita kaka yake na kumwambia ‘ninakufa naomba nisaidie kunitunzia mke wangu na watoto pia’, akakata roho,” alisema Mchungaji Opio.
0
UKIMWULIZA msanii wa kike anakutana na changamoto gani kwenye kazi yake ya sanaa, pamoja na nyingine wengi watakutajia kusumbuliwa kimapenzi. Naomba niweke wazi mapema, kuna tofauti kati ya kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na kutakiwa kutoa rushwa ya ngono. Hapa nazungumzia usumbufu wa rushwa ya ngono. Hiyo imekuwa kero kubwa kwa wasanii wa kike. Utakuta msanii ana kipaji kikubwa sana cha kuigiza, lakini anakutana na kikwazo hiki. Hakuna kupewa roll kubwa kwenye muvi mpaka atoke na director. Kwenye muziki kilio ni hichohicho. Msanii anahangaika kufanya mazoezi, anasaka pesa ya kurekodi na kwenda studio. Akifika huko anaweza kukutana na prodyuza mroho akamsumbua. Asipokutana na mtayarishaji msumbufu basi kuna kikwazo kwa staa anayetaka kumshirikisha kwenye ngoma yake. Mwanzo atajifanya ana lengo la kumsaidia kwenye singo yake tena bila malipo yoyote. Watakutana, watashirikiana kuandika mistari, watafanya mazoezi pamoja nk, lakini ikifika siku ya kuingiza vocal ataanza visingizio na mwisho wa siku atataka kutoka na msanii husika. Akipenya hapo, ngoma ikitoka atakutana na watangazaji wenye tabia hizo na huko watamwekea kauzibe. Akiona inakuwa ngumu, anaweza kuamua kwenda kwenye magazeti – atakutana na mambo hayohayo. Kama sivyo basi atatakiwa atoe fedha. Hapo ndiyo unakuwa mwisho. Stori ni hiyohiyo hata kwenye filamu. Msanii anacheza filamu moja, kisha ndiyo imetoka. Asilimia kubwa ya waliongia kwenye mkumbo wa namna hiyo wameishia pabaya. Wamepoteza nafasi za kutoka na vipaji vyao pia vimefia hapo. Lakini pamoja na changamoto hiyo kuwa kikwazo na kuwarudisha nyuma wasanii wa kike tatizo kubwa ni kutojiamini. Orodha ya wasanii wa kike walioamua kuachana na sanaa au sanaa kuwaacha baada ya kudanganyika ni ndefu,  nawapongeza sana wale waliojitahidi na kushikilia misimamo yao. Wapo wasanii wa mfano ambao tunao kwenye sanaa na mpaka sasa wanafanya vizuri. Lady Jaydee ni miongoni mwao. Alianza kuvuma mwaka 2000 (miaka 17 iliyopita) na mpaka sasa yupo kwenye game. Hebu jiulize, wasanii walioanza muziki na Stara Thomas  waliishia wapi? Wako wapi walioingia kwenye uigizaji na kina Monalisa, Thea na Johari? Tatizo ni kutojiamini. Wasanii wa kike msikubali kutumiwa na waroho, wasio wastaarabu na wasioheshimu thamani ya mtoto wa kike. Mkijiamini na kushikamana mtaweza kushinda kizingiti hicho.
1
NA MOHAMED KASSARA-DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa Alliance FC, Athumani Bilal ‘Bilo’ amesema licha ya kuridhishwa na kiwango kilichooneshwa na vijana wake katika michezo ya kirafiki waliocheza, atatumia muda mchache uliobaki kuongezea makali safu ya ushambulaji kabla ya kuivaa Mbao FC. Alliance inatarajia kucheza mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara Agosti 24, mwaka huu dhidi ya Mbao FC, Uwanja wa Kirumba, Mwanza. Timu hiyo imetoka kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya  Pamba,  inayoshiriki Ligi  Daraja Kwanza (FDL) na kulazimishwa sare ya bao 1-1, wiki iliyopita. Akizungumza na MTANZANIA jana, Bilo alisema kuwa amefurahishwa na viwango vya wachezaji, lakini atalazimika kusuka upya safu ya ushambuliaji kwa ajili kuhakikisha inafunga mabao mengi. “Ni kweli kabisa vijana wangu wapo katika kiwango bora, wanacheza kwa ushirikiano mkubwa na kila mmoja ana morali ya juu, hali hii inanipa imani kuwa tutakuwa na msimu mzuri. “Lakini kabla ya kucheza na Mbao, nitaisuka upya safu ya ushambualiaji ili iweze kutumia nafasi zinazopatikana, mpango huo ukikamilika usishangae kusikia tukimpiga nyingi, kwani vijana wako moto sana,”alisema Bilo.  
4
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao  Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40)  na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele  ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa  kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020  maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam  kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu.
5
Rais John Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa familia zilizopoteza jamaa zao katika ajali ya barabarani iliyotokea jana (Februari 21, 2019 Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe na kuua abiria 19. Taarifa kutoka Ikulu iliyosambazwa kwa vyombo vya habari leo Ijumaa (Februari 22, 2019) imeeleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana (Alhamisi) majira ya saa 3:15 usiku katika mteremko wa mlima Senjele baada ya lori lililokuwa likisafiri kutoka Tunduma kwenda Mbeya Mjini kugonga basi la abiria kwa nyuma ambalo liligonga lori jingine na kuminywa katikati.  Rais Magufuli amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen.Mstaafu Nicodemas Mwangela kufikisha salamu zake za pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na vifo vya watu hao na amewaombea kwa Mwenyezi Mungu aziweke roho za Marehemu wote mahali pema peponi, Amina. “…Rais Magufuli amezitaka mamlaka zinazohusika na usalama wa barabarani Mkoani Songwe kufanya uchunguzi wa ajali hiyo na kuchukua hatua zinazostahili pamoja na kujipanga vizuri kukabiliana na matukio ya ajali za barabarani,” taarifa hiyo imemnukuu Rais Magufuli. Wakati huo huo, Dk Rais Magufuli ametoa mkono wa pole kwa familia ya Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla ambaye amefiwa na mwanae aitwaye Zul Hamis Kigwangalla jana (tarehe 21 Februari, 2019), jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Magufuli akiwa na mkewe, Janeth wamefika nyumbani kwa familia hiyo, Mikocheni, jijini Dar es Salaam na kukutana na baadhi ya wanafamilia wakiongozwa na mama wa Marehemu, Dkt. Bayoum Kigwangalla ambao walikuwa katika maandalizi ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Nzega mkoani Tabora.
3
["Mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or kwa mwaka 2019 si mwingine bali ni Lionel Messi, ambaye amejichukulia kinyang'anyiro cha kuwa mchezaji bora zaidi kwa mara ya sita.", 'Mchezaji huyo wa Argentina mwenye miaka 32 amenyakua tuzo hiyo baada ya kuikosa toka mwaka 2015 na hii ni kutokana na kuweza kufunga mara 54 katika klabu ya nchini kwake kwa mwaka 2018-19 .', 'Virgil van Dijk alikuwa mshindi wa pili - yeye ni miongoni mwa wachezaji wanne wa Liverpool katika saba bora, akiwemo Sadio Mane.', 'Mchezaji wa Juventus Cristiano Ronaldo, aliwahi kutunukiwa tuzo hiyo mara tano na amekuwa watatu katika kura.', 'Toka mwaka 2008 tuzo hiyo maarufu zaidi ya wasakata kandanda duniani imetawaliwa na washambuliaji hatari katika kizazi cha sasa Messi na Ronaldo. ', 'Mpaka kufikia mwaka 2017, kila mmoja wao akishinda mara tano. ', 'Kiungo wa Real Madrid na timu ya taifa la Croatia Luka Modric aliingilia ufalme wa Messi na Ronaldo baada ya kunyakua tuzo hiyo mwaka jana. ', 'Na sasa Messi amerejea kileleni kwa kumpiku Ronaldo na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kunyakua tuzo hiyo mara sita. ', 'Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa mwaka huu kwa Messi, Ronaldo na Van Dijk kuwania tuzo moja kwa pamoja.', 'Mara ya kwanza walikutana katika tuzo za Mchezaji Bora wa Ulaya (Uefa) mwezi Agosti ambapo Van Dijk aliibuka na ushindi. ', 'Mara ya pili wakaminyana katika tuzo za Mchezaji Bora wa Fifa ambapo Messi aliibuka mshindi.', "Tano Bora ya Ballon d'Or", '1. Leonel Messi (Barcelona na Argentina)', '2. Virgil van Dijk (Liverpool na Uholanzi)', '3. Cristiano Ronaldo (Juventus na Ureno)', '4. Sadio Mane (Liverpool na Senegali)', '5. Mohammed Salah (Liverpool na Misri)', "Ballon d'Or ni nini?", "Tuzo ya Ballon d'Or imekuwa ikitolewa nchini Ufaransa kila mwaka toka 1956, na mshindi wake wa kwanza alikuwa mchezaji kutoka Uingereza Stanley Matthews.", 'Awali tuzo hiyo ilikuwa ni kwa wachezaji wa Ulaya tu kabla ya kufanyika mabadiliko mwaka 1995 na kujumuisha wachezaji wa mataifa yote duniani, mradi wanasakata kandanda katika vilabu vya Ulaya. ', 'Orodha ya majina ya wachezaji 30 bora huandaliwa na baadae kupigiwa kura na wanahabari wa michezo kutoka sehemu tofauti duniani, ambapo kila nchi hupiga kura moja. ', 'Kutoka mwaka 2010 mpaka 2015 tuzo hiyo iliunganishwa na ile ya Fifa lakini zilitengana mwaka 2016 ambapo Fifa ilianza kundaa tuzo zao wenyewe. ']
4
Na CHRISTOPHER MSEKENA STAA wa filamu za Kibongo Irene Uwoya, ameendelea kugonga vichwa vya habari za burudani baada ya mume wake, Hamad Ndikumana aliyefunga naye ndoa ya Kikristo kufariki dunia mapema wiki hii akiwa nyumbani kwake, Kigali nchini Rwanda. Kwa wiki tatu mfululizo Uwoya amekuwa hakuauki kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kwa tukio aliloliita ni ndoa ya Kiislamu aliyofunga na msanii wa Bongo Fleva, Abdulaziz  Chende ‘Dogo Janja’, ndoa ambayo Janjaro alithibitisha siyo filamu, licha ya Uwoya kudai ni filamu. Mfululizo wa tukio la ndoa mpya na msiba wa mume wake, Ndikumana yamepokewa kwa mitazamo tofauti na mashabiki wake. Wapo waliompa pole huku wengine wakimtusi. Wanaomtusi wanahusisha tukio lake la ‘ndoa tata’ na Janjaro kuwa huenda limemuumiza Ndikumana kiasi cha kupata mshtuko wa moyo na kupoteza maisha. Hata hivyo, kwa jumla wengi wameonyesha kuguswa na msiba huo na kuonyesha hisia zao. Katika kundi hilo ambalo lina watu wengi zaidi, wamekwenda mbali zaidi na kuumizwa kwa msiba huo kiasi cha kufananisha na pigo alilopata mzazi mwenzake na msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady baada ya kufiwa na aliyekuwa mumewe Ivan Don. NDOA Uwoya aliolewa na kocha huyo msaidizi wa Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda mwaka 2009 na katika maisha yao ya ndoa walifanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume   aitwaye Krish, ambaye amekuwa akiishi naye jijini Dar es Salaam. Upande wa Zari, naye alifunga ndoa ya kimila na mfanyabiashara wa Uganda, Ivan Ssemwanga ‘Ivan  Don’  miaka mingi iliyopita na katika maisha yao ya ndoa walifanikiwa kupata watoto watatu wa kiume. CHANGAMOTO NDANI YA NDOA Mwezi uliopita, Uwoya na mzazi mwezake marehemu Ndikumana, walianza kutupiana maneno kwenye mitandao ya kijamii ambapo Ndikumana alitoa malalamiko kwa mrembo huyo kuwa katika maisha yao hakuwa mkweli ikiwa ni pamoja na kumnyima haki ya kumsalimia mtoto wao, Krish anayeishi Bongo na yeye akiwa anaishi Rwanda. Malalamiko hayo, Uwoya aliyakanusha na zaidi aliendelea kufanya mitikasi yake ikiwa ni pamoja na kula bata nchini China hata aliporejea nchini, Octoba 27, mwaka huu akadai kufunga ndoa na Dogo Janja, jambo ambalo lilionekana kutomuumiza Ndikumana. Alichofanya Ndikumana ni kujibu mashambulizi kwa kumtangaza mpenzi wake mpya wa Kinyarwanda, aliyemtaja kwa jina la Asmah na kuendelea na maisha yake ya furaha huku akionyesha kutokuwa na presha na ndoa ya Uwoya na Dogo Janja kwani mrithi wake  aliweza kurudisha tabasamu lake lililopotea. Hiyo ilikuwa Oktoba 31, mwaka huu. Upande wa Zari, raia huyo wa Uganda aliachana na mume wake Ivan Don mwaka 2014 baada ya kunasa kwa staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ambapo mpaka sasa wamepata watoto wawili, Tiffah na Nillan. Zari alikuwa karibu mno na watoto wake aliozaa na Ivan Don licha ya vijana hao wa kiume kuishi na baba yao Uganda na Afrika Kusini lakini hakuwahi kuonyesha nia ya kumrudia mumewe zaidi ya kuboresha panzi lake jipya na Diamond Platnumz. Ivan Don kwa muda wote huo akiwa mbali na mke wake alionyesha kuwapenda watoto wake, kusimamia miradi yake iliyopo Afrika Kusini na Uganda pamoja na kula bata na kundi lake la Rich Gang bila kuwa karibu na mrembo mwingine. VIFO VYA WAUME ZAO Kifo cha Ndikumana kimetokea ghafla usiku wa kuamkia Jumatano ya wiki hii, akiwa nyumbani kwake. Inadaiwa alipata tatizo la maumivu ya kifua kabla ya mauti kumkuta. Siku nzima kabla ya kifo chake alikuwa mzima,  hata jioni yake alikuwa mazoezini akiwanoa wachezaji na yeye mwenyewe akishiriki mazoezi. Afisa Habari wa klabu hiyo aitwaye Gwakaya alisema Ndikumana alipata maumivu makali ya kifua na akaomba soda ya baridi, alipomaliza kunywa kidogo akatapika kisha akakata kauli hivyo anadhaniwa amekufa kwa ugonjwa wa moyo. Ndikumana ni baba wa watoto wawili wa kiume Baasit na Krish. Alizikwa Jumatano kwenye mjini Nyamirambo, Rwanda. Kifo cha Ivan Don, kilikuja baada ya tajiri huyo kuugua na Zari kushiriki katika kumuuguza kwenye Hospitali ya Stive Biko Academy, Afrika Kusini mpaka alipofariki kwa ugonjwa wa mshtuko wa moyo, Mei 25, mwaka huu na kuzikwa Nakarilo, Uganda. UWOYA AVISHWA VIATU VYA ZARI Kama unavyoona hapo juu, matukio yaliyotokea kwenye maisha ya Zari yanawiana kidogo na yale yaliyomtokea Irene Uwoya kwa kuwa wote waume zao wamepoteza maisha baada ya ndoa zao kuvunjika. Mungu ailaze roho ya marehemu Hamad Ndikumana mahali pema peponi – Amina.
1
MAHAKAMA ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara, imewahukumu raia watatu wa China kulipa faini ya Sh milioni 105 kila mmoja au kwenda jela miaka sita baada ya kukiri makosa mawili ya kusafi risha madini kwa nia ya kuyapeleka nje ya nchi bila ya kibali. Watuhumiwa hao walilipa faini na kuikwepa jela. Chini ya Hakimu Mkazi Veronika Mugendi, waliohukumiwa ni Yong zhe Ye (32), Chang Shaobo (31) na Xaolin Wang (25). Hata hivyo, dereva wao, Mtanzania Heneriko Shija (51), amebaki katika kesi hiyo baada ya kukanusha na shauri lake litatajwa Septemba 20, mwaka huu. Aidha mali ambazo ni dhahabu kilo 28.116, gari walilokuwa nalo, na mashine ya kufanyia utafiti zimetaifishwa na mahakama na kuwa mali ya umma. Kukamatwa kwa raia hao wa China wakitorosha madini kinyume cha sheria kwenda nje ya nchi,wanafikisha idadi ya raia wa nchi hiyo kukamatwa wilayani Tarime kuwa 6 katika kipindi cha mwezi mmoja. Wengine waliokamatwa awali na kufikishwa mahakamani hapo hivi karibuni ni Li Ninghi, Wang Xialong na Wang Zungsong ambao walikamatwa na vifurushi tisa vyenye kilo 300.75 za madini yakiwemo ya dhahabu wakiwa na gari aina ya Toyota Landcruiser VX V8 yenye namba za usajili KBW 515 L wakishtakiwa kwa makosa mawili ya kusafirisha madini bila kibali na uhujumu uchumi. Katika kosa la kwanza kila mmoja alihukumiwa kulipa faini ya Sh milioni 5 ama kifungo cha mwaka mmoja na kosa la pili kulipa faini ya Sh milioni 100 ama kifungo cha miaka 5. Walilipa faini, gari na madini vilitaifishwa. Katika kesi ya uhujumu uchumi namba 51/2019 iliyotolewa hukumu juzi Septemba 6 na Hakimu Mugendi ya Wachina hao wengine watatu Yongzhe Ye, Chang Shaobo na Xaolin Wang, walikiri mashitaka yao mawili ya kusafirisha madini bila kibali na uhujumu uchumi. Walikuwa wakitetea na Mwanasheria Joseph Mugabe. Awali wanasheria wa Serikali, Venance Mayenga na Aininus Kainunura walidai mahakamani hapo kuwa Wachina hao wamekuwa wakijishughulisha na utafiti wa madini katika maeneo ya Nyasirori Wilaya ya Butiama.Walidai Agosti 12, mwaka huu saa 3 usiku katika kizuizi cha Komaswa barabara kuu ya Musoma kwenda Sirari wakiwa na gari aina ya Toyota Hilux yenye namba T 994 DHC wakiwa wamefunika matunda aina ya matikiti, walikamatwa na vifurushi 21 vya madini na chupa mbili wakisafirisha kinyume cha sheria bila ya kuwa na vibali vya kusafirisha madini hayo kwa nia ya kuyapeleka nje ya nchi bila kufuata utaratibu
3
Ramadhani Hassan -Dodoma SERIKALI imewataka wamiliki wa shule wote kutumia busara kutowarudisha wanafunzi nyumbani pindi shule zitakapofunguliwa kwa wazazi wao kutokuwa na ada. Ushauri huo ulitolewa jana jijini Dodoma na Waziri wa  Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza na waandishi wa habari kutangaza ratiba za mitihani ya kitaifa. “Wito kwa wamiliki wa shule kutumia busara kudai ada, shule zimefunguliwa ghafla, naamini baadhi ya wazazi walikuwa hawajipanga. “Tuwe na moyo wa kupendana, wale ambao hawana ada tuweke ubinadamu ila na wale ambao hawajalipa kipindi ambacho kulikuwa kuna ugonjwa wa corona walipe. “Sio vizuri kumkatalia mtoto wa masikini asiendelee na masomo, naamini kamati za shule zitakaa na kuweka utaratibu sawa,” alisema Profesa Ndalichako. RATIBA YA MITIHANI Katika hatua nyingine, Profesa Ndalichako alitangaza rasmi tarehe za mitihani ya taifa kwa watahiniwa  wa mwaka huu na mihula ya masomo kwa shule zote nchini. Profesa Ndalichako alisema baada ya tangazo la Rais Dk. John Magufuli juzi wakati akivunja Bunge kuagiza masomo kuanza Juni 29, wizara yake imelipokea. Alisema ratiba za mitihani kwa darasa la saba (PSLE) itafanyika kuanzia Oktoba 7 hadi 8. Profesa Ndalichako alisema kidato cha pili (FTNA), itakuwa  kuanzia Novemba 9 hadi20, kidato cha nne (CSEE) kuanzia Novemba 23 hadi Desemba 11 na darasa la nne (SFNA) kuanzia Novemba 25 na 26. Alisema  kwa shule za msingi na sekondari, wanafunzi watarejea shuleni Juni 29 na kumaliza muhula wa kwanza wa masomo Agosti  28, na kuanza muhula wa pili ambao utaisha Desemba 18. Profesa Ndalichako alisema kwa wanafunzi wa kidato cha tano nao wataripoti shuleni Juni 29 kama ilivyotangazwa, na watasoma na kukamilisha muhtasari wa kidato cha tano na mitihani iifikapo Julai  24. Alisema wataanza rasmi masomo ya kidato cha sita Julai 27. “Niwasihi na kuwaomba wanafunzi wote kusoma kwa bidii, hatutakuwa na likizo, itakuwa ni kusoma tu labda mwezi wa nane watapumzika kidogo, lakini wataendelea na masomo kwa sababu wamepumzika muda mrefu kutokana na janga la ugonjwa wa corona,” alisema Profesa Ndalichako. Alisema wizara inasisitiza uongozi wa shule zote nchini kuhakikisha wanafunzi, walimu na wafanyakazi wasio walimu wanazingatia maelekezo ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ya ugonjwa wa corona.  “Ninaomba niwatoe shaka, hakuna mwanafunzi yeyote aliyeugua corona mara baada ya kuwaruhusu kurudi shule,” alisema Profesa Ndalichako. Alisema ili kukamilisha muhtasari wa masomo, shule zitalazimika kuongeza saa mbili za masomo kwa siku ili kufidia muda uliopotea..
3