text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
BANGKOK, Thailand NYOTA wa muziki nchini Marekani, Jay Z, amempeleka mwanawe nchini Thailand kwa ajili ya kuangalia makumbusho nchini humo. Jay Z aliungana na mke wake, Beyonce na mtoto wao, Blue Ivy kwa ajili ya kumuonesha makumbusho mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kuufurahia mwaka 2015. Baada ya kuwasili katika makumbusho ya Fantasea nchini humo, alikutana na Chui ambaye alikuwa anang’ara kwa rangi ya dhahabu huku ikiwa sawa na rangi ya nguo ambayo alivaa mtoto huyo, hali hiyo ilimfanya mtoto huyo kung’ang’ania mahali alipo mnyama huyo kwa muda mrefu. Mtoto huyo kwa sasa amekuwa ni miongoni mwa watu waliotembea maeneo mbalimbali duniani. , amempeleka mwanawe nchini Thailand kwa ajili ya kuangalia makumbusho nchini humo. Jay Z aliungana na mke wake, Beyonce na mtoto wao, Blue Ivy kwa ajili ya kumuonesha makumbusho mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kuufurahia mwaka 2015. Baada ya kuwasili katika makumbusho ya Fantasea nchini humo, alikutana na Chui ambaye alikuwa anang’ara kwa rangi ya dhahabu huku ikiwa sawa na rangi ya nguo ambayo alivaa mtoto huyo, hali hiyo ilimfanya mtoto huyo kung’ang’ania mahali alipo mnyama huyo kwa muda mrefu. Mtoto huyo kwa sasa amekuwa ni miongoni mwa watu waliotembea maeneo mbalimbali duniani.
1
MWENYEKITI wa Yanga SC, Dk Mshindo Msolla amekiri wachezaji wa timu hiyo hawajalipwa mishahara ya miezi miwili na kwamba walitarajiwa kuwaingizia kwenye akaunti zao jana.Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Jwangani na Twiga jana, Msolla alisema hicho ndio chanzo cha baadhi ya nyota wake wa kimataifa kuandika barua za kuvunja mikataba.Alisema wanachama na wapenzi wa timu hiyo wanapaswa kujua bado hali ya uchumi kwa sasa si shwari kwani mapato wanayoingiza ni Sh bilioni 2 .2 kwa mwaka, kiasi alichodai ni kidogo kulinganisha na matumizi ya timu ambayo ni Sh bilioni nne kwa mwaka.Alisema, tangu uongozi wake uingie madarakani ulikuta madeni yenye thamani ya Sh bilion mbili ambayo wameanza kupunguza kulipa kidogo kidogo ikiwemo kwa makocha wa zamani wa timu hiyo akiwemo Hans Van Pluijm (Sh milioni 22), George Lwandamina (Sh milioni 25) na Juma Mwambusi.Kuhusu wachezaji wa zamani wanaodai mpaka sasa ni Donald Ngoma, Youth Rostand, Obrey Chirwa, Thaban Kamusoko na watu binafasi Sh milioni 217. “Hayo madeni yote ya wachezaji na makocha ukijumlisha unapata Sh milioni 600,” alisema.“Ni kweli wachezaji wetu hawajalipwa mishahara zaidi ya miezi miwili sasa na kuna mchezaji kama Sudney Ulikhob (Namibia) tumeachana naye kwa amani kabisa aliandika barua ya kuomba kuvunja mkataba, mchezaji Lamine Moro (Ghana) alileta barua ya kufanya hivyo lakini tulipanga kukutana naye siku ya pili yake lakini tulipomtafuta alionekana kasharudi kwao Ghana.”“Tumeahidi kwamba tutamalizana naye muda wowote kuanzia leo (jana) kwa kumlipa mshahara wake ili aendelea kuitumikia Yanga kwa hiyo mashabiki wawe na amani,” alisema Msolla.Pia Msolla alisisitiza mchezaji, David Molinga bado hajaandika barua yoyote kuufikishia uongozi wa timu hiyo kuomba kuvunja mkataba kama inavyodaiwa.Alisema katika timu hiyo, hakuna fedha inayoibiwa isipokuwa matumizi yamekuwa makubwa kuliko kiasi cha fedha wanachoingiza na kwamba kwenye michezo miwili ya Ligi Kuu iliyochezwa Dar es Salaam walivuna Sh milioni nane, fedha ambazo ni ndogo kulinganisha na gharama za uendeshaji wa timu.Msolla pamoja na kukiri hali hiyo mbaya ya kiuchumi, alisema kipaumbele cha uongozi wa timu hiyo kwa sasa wanajikita kwenye kutoa huduma kwa wachezaji wa vikosi vyote ikiwemo Yanga Princess, wafanyakazi wote na timu ya vijana kwa kuwasafirisha kwenda kucheza mechi na mahitaji mengine muhimu.
4
Hayo yalisemwa na mtaalamu wa madini ya vito na almasi kutoka Kitengo cha Uthamini wa Madini ya Vito na Almasi (TANSORT) kilicho chini ya Wizara ya Nishati na Madini, Teddy Goliama kwenye semina iliyoshirikisha Makamishna Wasaidizi wa Madini wa Kanda, Maofisa Madini Wakazi na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini inayoendelea mjini Bagamoyo.Goliama alisema Tanzania kupendekezwa kuwa kitovu kikuu cha madini ya Tanzanite ni matunda ya ziara iliyofanywa na Kitengo cha TANSORT kwa kushirikisha wataalamu wa wizara ikiwa ni pamoja na ushiriki wake katika Maonesho ya Kimataifa ya Vito ya Thailand yajulikanayo kama Bangkok Gem and Jewellery Fair.Alisema sababu zilizopelekea Tanzania kupendekezwa kuwa kitovu cha biashara ya madini ya vito Afrika ni kutokana na wingi na aina mbalimbali za madini hayo pamoja na madini hayo kupendwa na wafanyabiashara wengi kutoka Thailand na nchi nyinginezo duniani.Alisema awali Waziri Mkuu wa Thailand aliitembelea Tanzania na kukutana na Serikali na wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini na kukubaliana maeneo ya kushirikiana ambapo aliahidi kuisaidia Tanzania katika kukuza biashara ya madini ya vito.Goliama aliendelea kusema kuwa Waziri Mkuu huyo aliikaribisha Tanzania kutembelea Thailand pamoja na kukutana na wataalamu wa sekta wa madini wa nchi hiyo ambapo ujumbe wa wataalamu wa madini ukiongozwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Stephen Maselle ulitembelea nchi ya Thailand na kukutana na uongozi wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Thailand unaoshirikiana na Serikali ya Thailand bega kwa bega.Alisema kuwa moja ya mikakati ya kukuza biashara ya madini ya vito iliyowekwa ilikuwa ni kutoa fursa kwa Tanzania kushiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Vito huko Bangkok ambayo hufanyika mara mbili kwa mwaka, Februari na Septemba.Alisisitiza kuwa, baada ya Tanzania kufanya vizuri katika maonesho hayo na kubainika kuwa na hazina kubwa ya madini ya vito ilipendekezwa kuwa kitovu cha biashara ya madini hayo barani Afrika.
5
    Na Christian Bwaya, MARA nyingi tumesikia watu wakilaumu mtalaa wetu kwamba unafunga fahamu za wanafunzi wetu. Wenye madai haya wanafikiri bila mtalaa kufanyiwa marekebisho makubwa, haiwezekani elimu yetu ikamnufaisha mwanafunzi. Hata hivyo, tulisema wiki iliyopita, kazi ya mtalaa ni kutoa dira ya jumla ya aina ya raia wanaotarajiwa kufundwa kupitia mtalaa husika. Mwalimu ndiye mwenye kazi kubwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wanaelewa kile kinachokusudiwa kufikiwa na mtalaa. Katika makala haya ninalenga kuonesha namna gani mwalimu aliyefuzu anaweza kutumia mtalaa huu unaolalamikiwa kujenga tabia ya udadisi kwa wanafunzi wake. Ningependa nitumie mfano wa Shirika lisilo la Kiserikali liitwalo Opportunity Education. Shirika hili linaendesha mradi unaoitwa Next Generation Learning (NGL) ambao kimsingi unajaribu kutafsiri maudhui ya mtalaa katika mazingira halisi ya mwanafunzi. Kazi hii inafanywa na walimu wa shule zetu waliopata mafunzo maalum kuandaa mfululizo wa masomo yanayoandaliwa kutokana na mtalaa wetu. Sambamba na kutafsiri maudhui ya mtalaa wetu, NGL wametengeneza mfumo wa ufundishaji na ujifunzaji wanaousimamia wao wenyewe kwenye shule teule. Mradi huu ambao tayari umeshaonesha mafanikio, unatumia kanuni kuu tano ambazo naamini mwalimu yeyote anaweza kuzitumia. Kwanza, kuhakikisha kuwa mwanafunzi anaelewa kwa nini anahitaji kujifunza kile anachojifunza. Hili kwa hakika limekuwa changamoto ya ufundishaji wa kimazoea. Tumekuwa tukifundishwa maudhui ambayo kwa kweli hatuelewi tutayatumia wapi. Nakumbuka kwa mfano, nikiwa kidato cha V kwenye somo la Fizikia tulifundishwa hesabu ndefu za namna ya kutafuta muda utakaotumiwa na tone la mwisho kudondoka kwenye bomba la maji linalofungwa. Hatukuelewa kwa nini ilikuwa ni lazima kusumbua akili kufanya hesabu hizi ngumu zisizotatua tatizo lolote kwenye maisha yetu. Ufundishaji wa namna hii, kwa hakika, unamkatisha tamaa mwanafunzi. Mwanafunzi asiyeelewa kwa nini anasoma kitu hawezi kuwa na udadisi. NGL wameonesha mfano wa namna tunavyoweza kuondoa hitilafu hii. Kupitia mfumo wao wa ujifunzaji, NGL wanajaribu kufikiri namna gani kile kinachofundishwa kinagusa maisha ya kawaida ya mwanafunzi. Kujua uhusiano wa maudhui na maisha yake kunamwongezea mwanafunzi ari ya kujifunza kwa sababu anaelewa thamani ya kile anachotarajiwa kujifunza. walimu anapata somo muhimu hapa. Kwamba ni muhimu atafute namna ya kuhusianisha somo lake na maisha ya mwanafunzi. Kwa mfano, mwalimu wa Kemia anapofundisha somo la Mada (matter) anahitaji kufanya kazi ya ziada kumsisimua mwanafunzi kuona namna maarifa ya mada yanavyoweza kumsaidia katika maisha yake ya kila siku. Kazi hii haifanywi na mtalaa bali mwalimu. Kanuni ya pili inayotumiwa na NGL, ni kuhakikisha mwanafunzi anajenga uwezo wa kujiuliza maswali ya msingi kuhusu hicho anachojifunza badala ya kutegemea majibu yaliyopikwa na mwalimu anayeonekana kuwa mjuzi na mmiliki wa maarifa. Kwa hakika madarasa yetu yanafanya kinyume. Kazi ya walimu imekuwa ni ‘kuhubiri’ maarifa kwa mwanafunzi. Mwanafunzi anachukuliwa kama mtu anayesubiri kupikiwa kila kitu na kazi yake ni ‘kumeza’ kile anachoambiwa. Hana fursa ya kuuliza wala kuhoji. Shule zetu ‘zinazofaulisha sana’ kimsingi zinajitahidi kuhakikisha mwanafunzi anafahamu kwa hakika nini cha kukariri. Walimu wa shule hizi wanafanya bidii kubwa kuwaimbisha wanafunzi kile wanachojua kitaulizwa kwenye mtihani. Somo tunalopewa na Opportunity Education ni kwamba mwanafunzi anayewekewa mazingira ya kujiuliza maswali na kushiriki moja kwa moja katika kutafuta majibu, anakuwa na uwezo wa kudadisi kuliko mwenzake anayeshiriki ‘kumeza’ maarifa. Mwalimu lazima afanye kazi kubwa ya kuibua maswali yanayohusiana na kile anachokifundisha ili wanafunzi waweze kujifunza kwa mfumo wa kutafuta majibu wao wenyewe. Mradi wa NGL unatuthibitishia kuwa mwalimu akiwezeshwa anaweza kutafsiri mtalaa huu unaodaiwa kuwa haufai kuibua kiu ya kutafuta majibu. Kanuni ya tatu ni kumtarajia mwanafunzi kutumia maarifa yake kutengeneza ujuzi. Mwanafunzi wa NGL si tu anahitajika kujibu maswali ya kufikirisha, bali kuonesha ujuzi mahususi. Mathalani, baada ya mwanafunzi kujifunza namna mimea inavyotengeneza sukari kwa kutumia mwanga wa jua, lazima aoneshe anavyoweza kutumia maarifa hayo kutatua matatizo katika mazingira yake. Inaendelea Mwandishi ni Mhadhiri wa Saikolojia katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU).  Blogu: http://bwaya.blogspot.com, 0754870815
3
Akizungumza na gazeti hili Kabange alisema katu haamini kama ushirikina unaweza kuinua soka la Tanzania, bali uwezo wa wachezaji pekee ndio ambao unahitaji kuangaliwa.“Mimi siamini ushirikina kama ndio unaobeba soka, kama wapo wanaotumia kujiinua ni sawa na bure, waonyeshe kiwango chao ndipo tutaona uwezo wao,” alisema Kabange.Alisema timu yake imekuwa ikifanya vizuri sio kwasababu ya ushirikina isipokuwa wachezaji hujituma na kuonesha kiwango cha hali ya juu ndio maana wamepata mafanikio.Kagera Sugar imekuwa ikifanya vizuri katika michezo ya nyumbani na ugenini na kufikisha pointi 14, kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.Kikosi hicho kinatarajiwa kucheza na Mbeya City mwishoni mwa wiki hii katika mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba ambapo Kagera itakuwa ikiutumia kama uwanja wa nyumbani baada ya ule wa Kaitaba kuwa kwenye ukarabati.Akiizungumzia Mbeya City, Mrage alisema sio timu ya kubeza kwani wachezaji ni wazuri na wamekuwa wakijitahidi hivyo watapambana katika kugombea nafasi za juu.Alisema ushindi ni muhimu kwao katika mchezo huo na kuahidi mashabiki kuutumia uwanja wao wa nyumbani katika kusaka pointi tatu.
4
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imeahidi kutatua changamoto zinazokabili vyama vya ushirika ikiwemo kushughulikia viongozi wabadhirifu, hali inayopelekea vyama vya ushirika kutoaminiwa na wananchi. Akizungumza bungeni leo Waziri wa Kilimo Hussein Bashe ameeleza kuwa serikali imekuwa ikitekeleza mikakati mbalimbali yenye lengo la kurudisha ubora wa vyama vya ushirika ikiwemo uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya akiba na mikopo (SACCOS), sambamba na kuhamasisha vikundi vya vijana na akina mama vyenye muelekeo wa ushirik.Waziri Bashe ameyabainisha hayo leo Jumanne, Septemba 10, 2019 alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti maalumu Amina Makilagi kuhusu hatua ambazo serikali imechukua kuhakikisha vyama hivyo vinaleta tija kwa wakulima mbalimbali nchini. “Ushirika ni utelelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi ya meaja 2015-2020 kama ilivyoainishwa katika ibara ya 22 kifungu F, G na H kuwa ushirika ndio suluhu pekee inayoweza kukwamua mkulima mdogo kupitia kuungana na kutengeneza chombo imara cha kuwatetea” amesema. Waziri Bashe amebainisha kuwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika hususani kwenye mazao ya pamba, kahawa, miwa na ufuta wamekosa uadilifu, hali inayopelekea malengo mahususi ya uwepo wa vyama hivyo kutoonekana kutokana na vitendo vya ubadhirifu wa rasilimali za ushirika.  
3
WASHINGTON, MAREKANI RAIS Donald Trump amesema mashambulizi ya sumu nchini Syria yamebadili mtazamo wake kuhusu utawala wa Rais Bashir al Assad. Kabla na baada ya kuingia madarakani, Rais Trump aliahidi kuimarisha ushirikiano na Rais wa Urusi, Vladimir Putin ambaye ni mshirika wa karibu wa Rais al-Assad. Trump alikuwa akisema jitihada za Marekani nchini Syria zitalenga zaidi kupambana na kundi la kigaidi linalojiita Dola la Kiislamu (IS). Lakini hilo limebadilika baada ya kusambaa kwa video zinazoonyesha watoto wa Syria wakihangaika kupumua, wakitokwa na mapovu mdomoni huku wakionekana kuwa na maumivu makali. Trump alisema shambulio hilo halivumiliki na limevuka mipaka. Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Nikki Haley, ameonya Marekani inaweza kuchukua hatua peke yake. “Umoja wa Mataifa unaposhindwa kutimiza jukumu lake la kuchukua hatua, inabidi sisi wenyewe tuingilie kati,” alisema Haley. Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson, alisisitiza kuitaka Urusi kufikiria upya ushirikiano wake na Serikali ya Assad. Serikali ya Syria hata hivyo imekana kuhusika na shambulio hilo la gesi yenye sumu, ikisema ni propaganda za wapinzani wake kuwachafua na kusisitiza lilifanywa na magaidi.
2
Na JUDITH NYANGE-MWANZA JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza linawashikilia watu saba kwa tuhuma za kukutwa na kete 32 za dawa za kulevya zinazodhaniwa kuwa ni heroine, kilo mbili na nusu za bangi na misokoto 75. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema watuhumiwa hao walikamatwa Februari 22, mwaka huu saa nne asubuhi maeneo ya katikati ya jiji na wote wakiwa ni wakazi wa Nyamagana. Msangi alisema kabla ya kuwakamata watuhumiwa hao walipokea taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu uwepo wao na walianza kuwafuatilia. “Watuhumiwa tuliowakamata ni Mago Ailaa (29) mkazi wa Mabatini, Emmanuel Marco (24) mkazi wa Bugarika, Josiah Leornad (30) mkazi wa Kirumba, mwanafunzi Allan Marwa (19), Fikiri Msafiri (36), Izack Anderson (31) mkazi wa Igogo, na Omari Ally(27) mkazi wa Mabatini, hao wote wanashikiliwa na polisi kwa kosa la kupatikana wakiwa na dawa za kulevya zinadhodhaniwa kuwa ni heroine zikiwa kete 32, bangi kilo moja na nusu na misokoto 75,” alisema Msangi. Alisema polisi inaendelea kuwafanyia mahojiano ili kubaini mtandao wa watu wanaoshirikiana nao katika biashara hiyo na uchunguzi utakapokamilika watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani. Alitoa wito kwa wakazi wote wa Mwanza kuendelea kutoa ushirikiano na taarifa za watumiaji, wauzaji na wasafirishaji wa dawa ya kulevya ili waweze kudhibitiwa.
3
Na GLORY MLAY-DAR ES SALAAM BINGWA wa mashindano ya soka ya makampuni yaliyoandaliwa na Benki ya Standard Chartered, TBL FC, inatarajiwa kuondoka Septemba mwaka huu kuelekea nchini Uingereza, kutembelea klabu maarufu ya Liverpool pamoja na  kukutana na wachezaji mashuhuri wanaoichezea klabu hiyo. Timu hiyo itakuwa nchini Uingereza kati ya Novemba 8 hadi 10, mwaka huu na itashuhudia mechi ya mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza, kati ya  timu ya Fullham na Liverpool utakaopigwa katika Uwanja wa Anfield. Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Group, Roberto Jarrin, aliipongeza Benki ya Standard Charted nchini kwa ubunifu mkubwa  wa kuwaunganisha wateja wake kupitia nyanja ya michezo sambamba na utoaji huduma bora kwa wateja wake. Naye, nahodha wa timu hiyo, Lupa Mwanjopa, alieleza kuwa wamefurahi kupata fursa hiyo ya kwenda nchini Uingereza sambamba na kutembelea klabu ya Liverpool na kukutana na wachezaji nguli wa timu hiyo. Mkuu wa Uhusiano na Masoko wa Benki hiyo, Juanita Mramba, alisema mbali na kutembelea klabu hiyo, pia watapata nafasi ya kufanya mazoezi katika Uwanja wa Anfield pamoja na kwenda kuangalia mchezo wa wapinzani wa Liverpool.
4
GRACE SHITUNDU, DAR ES SALAAM MWAKILISHI wa Jimbo la Shaurimoyo (CCM) Hamza Hassan Juma amewasilisha hoja binafsi  katika Baraza la Wawakilishi itakayowabana wanachama wapya kupewa nafasi ya kuwania  nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo urais. Hoja hiyo ambayo iliwasilishwa jana mbali na urais pia inaweka kikwazo kwa wagombea ubunge, uwakilishi na udiwani  kuwania nafasi hizo kabla ya kutimiza miaka miwili ya uwanachama katika chama chochote. MTANZANIA Jumamosi lilimtafuta Hamza na katika mahojiano yake na gazeti hili amedai kuwa endapo hoja yake hiyo itajadiliwa na kupitishwa  katika baraza hilo itapunguza pia utapeli wa kisiasa unaofanywa na baadhi ya wanasiasa wa kuhamahama vyama. Taarifa za kupelekwa kwa hoja hiyo binafsi, imezua mijadala katika mitandao mbalimbali ya kijamii huku baadhi ya wadau wa mambo ya siasa wakidhani kuwa ni ajenda ya chama tawala kutaka kuwabana wapinzani visiwani humo. Ikumbukwe ni hivi karibuni tu aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharrif  Hamad alikihama chama hicho sambamba kundi kubwa wa wafuasi wa chama hicho na kuhamia chama cha ACT Wazalendo. Inahofiwa kuwa endapo hoja hiyo binafsi ya Mwakilishi wa Shaurimoyo itajadiliwa na kupitishwa na wajumbe itakiathiri kwa kiasi kikubwa chama cha ACT Wazalendo ambacho kilijizolea wanasiasa wakongwe katika siasa za Zanzibar. Wanachama hao ndio wanaoonekana kuwa na nafasi kubwa ya kuleta upinzani mkali dhidi ya CCM katika kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka huu visiwani humo na hata kupewa nafasi kubwa ya ama kuchukua nafasi hiyo au kushiriki kwenye  Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Katika mahojiano yake na MTANZANIA Jumamosi Hamza alisema kuwa hoja hiyo haitawabana wanasiasa wa upinzani tu bali hata wale waliokuwa katika chama tawala. Alisema amepeleka hoja hiyo binafsi wa Spika wa Baraza la Wawakilishi amefuata utaratibu wote unaotakiwa ukiwemo kukitaarifu chama chake cha CCM. “Hii ni haki yangu kikatiba, kisheria na kikanuni kama mwakilishi ninaruhusiwa kupeleka hoja binafsi ninayoona inafaa katika Baraza la Wawakilishi. “Kwa sasa kumekuwa na tabia ya watu kupewa nafasi ya kuwania uongozi kupitia vyama ambavyo hawajavitumikia, hawajui misingi yake wala sera za chama hicho”, alisema. Aliongeza kusema, “Jumuiya ya Umoja wa Vijana katika chama chochote imewekwa kwa ajili ya kuwatengeneza kuwa viongozi wa baadae, lakini sasa kutokana na utapeli na tamaa za baadhi ya wanasiasa inafanya vijana hao kukosa nafasi wanazostahili”. Alisema katika miaka ya karibuni CCM imefanikiwa kupata wanachama wengi waliovihama vyama vyao na wengine walikuwa wabunge na madiwani ambao walipata tena nafasi ya kugombea tena nafasi hizo lakini endapo kungekuwa na masharti ya  ya kuwataka kutimiza miaka miwili wasingeweza kukubali kuhama. “Baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani walilalamika, kuwa CCM inawanunua wanachama hao ambao nao kwa upande wao hawakuwa na shaka wala hofu kwa kuwa walikuwa wanapewa nafasi ya kugombea tena nafasi zao,”alisema Hamza. Alisema  endapo kutakuwa na masharti kama hayo hakutakuwa na mtu wa kukubali kuhama chama na hivyo kupunguza chaguzi ndogo za mara kwa mara. “Mbowe (Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Chadema) na Zitto Kabwe (Kiongozi wa ACT-Wazalendo) walilamika sana sasa sisi tunawasaidia pia na wao katika hili kwani endapo itaendelea hivi unaweza kushangaa hata baada ya uchaguzi ujao mtu anahama tu baada ya mwaka hali ambayo inaongeza gharama zisizokuwa na sababu kwa Serikali” alisisitiza Hamza. Hamza alisema kwamba ameshapeleka hoja yake hiyo kwa Spika na anachosubiri kwa sasa ni lini Spika ataiweka kwenye ratiba. “Tayari imeshafika kwa spika na ninachosubiri ni maamuzi ya Spika yeye ndiye atajua ratiba, endapo muda utaruhusu kwa vikao hivi au vikao vijavyo”alisema Hamza. Uchaguzi katika visiwa vya Zanzibar unatarajiwa kuwa wa moto kutokana kwamba katika Uchaguzi mkuu huu Wazanzibar watachagua Rais atakayemrithi Dk. Mohamed Shein ambaye anamaliza vipindi vyake viwili baada ya kuiongoza Zanzibar kwa miaka 10. Pia vuguvugu la uchaguzi ni kubwa  baada ya mabadiliko makubwa yaliyotokewa katika chama kikuu cha upinzani kisiwani humo cha CUF.
3
MANISPAA ya Kigamboni imetoa mkopo yenye jumla ya Sh Milioni 300 kwa vikundi 88 vya wanawake, vijana pamoja na watu wenye ulemavu kwa ajili ya kujiendeleza katika shughuli mbalimbali za ujasiriamali.Fedha hizo ambazo zimekabidhiwa kwa vikundi hivyo juzi, kiasi cha Sh Milioni 200 zimetokana na marejesho ya mikopo iliyopita na kuifanya jumla ya mikopo iliyotolewa na manispaa hiyo kwa vikundi hivyo vyenye wanachama wapatao 880 hadi sasa kufikia kiasi cha Bilioni 1.3.Akizungumza wakati wa utoaji wa mikopo hiyo Mkurugenzi wa manispaa hiyo Ng’wilabuzu Ludigija alisema fedha hizo ni utekelezaji wa sera inayozielekeza kila manispaa kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya wanawake na vijana pamoja na watu wenye ulemavu.Alisema katika kuhakikisha wanaviinua kiuchumi vikundi hivyo, manispaa hiyo imeona vyema kuweka mazingira mazuri ya kuviwezesha vikundi kwa wakati huku akivipongeza kwa matokeo mazuri hususani katika urejeshaji wa mikopo hiyo.Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Sara Msafiri aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, mbali na kumpongeza mkurugenzi wa manispaa kwa utekelezaji mzuri wa sera ya utoaji wa mikopo kwa vikundi hivyo, alisema ni wajibu wa vikundi hivyo kuhakikisha wanazitumia fedha hizo vizuri ili kujiinua kiuchumi.
3
Iman Mketema Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amewaita Watanzania kujitokeza kwa wingi kuhudhuria tamasha Tanzania la Jamafest linalotarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 21 hadi 28, mwaka huu jijini Dar es Salaam . Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Septemba 18, Dk. Mwakyembe amesema lengo la tamasha hilo litakalofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ni kulinda na kuhifadhi na utamaduni wa kiafrika na kuweza kutambulika zaidi duniani. “Hii ni sherehe kubwa sana nchini kwetu kwani wazungu walivuruga utamaduni wetu enzi za utumwa na kupitia tamasha hili tunatunza utamaduni wetu,” amesema Dk. Mwakyembe. Amesema katika tamasha hilo kutakuwa na wimbo maalumu uliotungwa na msanii Peter Msechu akiwashirikisha wasanii wenzake Mimi Mars, Barnaba, Linah Sanga, Rich Mavoko na Khadija Kopa. “Lakini pia natoa nafasi ya kutumbuiza kwa msanii Nasibu Abdul (Diamond Platnumz) aje ajiunge na wasanii wenzake waweze kutumbuiza pamoja kwenye tamasha hilo kwani tamasha kama hilo lililofanyika Kenya niliona kulikwa na ushirikiano mkubwa baina ya wasanii hao nchini humo,” amesema Dk. Mwakyembe. Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Kiagho Kilonzo, alitangaza kuwa kutakuwa na tuzo za filamu kutoka bodi hiyo kwenye tamasha hilo. “Kutakuwa na tuzo tofauti tofauti kwenye tuzo hizo na ninawaomba wasanii wenye kazi zao wazilete ili zishindanishwe na washindi watatu watapatikana,” amesema Kilonzo.
3
BUNGE linaangalia uwezekano wa kuja na taratibu mpya za kutowadhamini wabunge kukopa benki hasa kutokana na wabunge wengi wa sasa kuwa na mzigo wa madeni na huwenda fedha hizo zikalipwa na fedha za umma.Aidha, wabunge wanane wa viti maalumu waliofukuzwa uwanachama na Chama cha Wananchi (CUF) na kupoteza sifa za kuwa wabunge wameacha madeni ya zaidi ya Sh bilioni moja yaliyotokana na mikopo waliyokopa.Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyasema hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake jana na kuongeza kuwa mingi ya mkataba ya mikopo iliyoingiwa na wabunge ina kasoro kadhaa. Ndugai alikuwa akijibu swali la waandishi wa habari kama Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) kama ni mbunge pekee ambaye amekopa.Alisema kuwa mbali na deni la zaidi ya Sh milioni 400 analodaiwa Lema baada ya kukopa Sh milioni 644, pia wabunge wanane wa CUF, waliofukuzwa na chama hicho kwa kumuunga mkono aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif, wanadaiwa zaidi ya Sh bilioni moja. Aidha, Ndugai alisema mbali na suala la ukopaji, pia Bunge linatarajia kupitia kanuni za Bunge ili kuhdibiti hali ya utovu wa nidhamu kwa wabunge.“ Kanuni hizo ziliweka hivyo zamani, hawa watu walikuwa ni waheshimiwa sasa wanakuja watu very much below (watu wa chini) wakati rules (kanuni) ni za waheshimiwa, namna ya kushughulikia inakuwa ngumu lakini tunapoelekea mwisho tutaziangalia hizi kanuni zote. Spika Ndugai aliongeza: “ Tulifikiria turekebishe hapo katikati lakini tutarekebisha kwa ajili ya bunge litakalofuata na tutaweka katika namna ambayo… tusiseme mapema lakini itatibu hii hali ya utovu wa nidhamu kwa makusudi na vurugu ambazo hazina tija kwa watanzania.“Wanaotetea acha watetee kwa sababu hawajui hali halisi kuwa mwisho wa siku lazima wayalipe hayo madeni ni hela yenu (fedha za serikali) ndio itakayotumika. Kuhusu suala la wabunge 8 wa CUF waliofukuzwa ubunge, Ndugai alisema: “ Huu ni mtihani mwingine tulionao, wabunge wale nane sijui ni 10? inadaiwa zaidi ya Sh bilioni 1 na hawana uwezo wowote wa kulipa.“Mikataba ile ipo hovyo hovyo kama watakazia wale jamaa (wakopeshaji) kuna kiwango fulani cha fedha ya walipa kodi inaweza kutumika kulipa madeni ya hovyo. Ndio maana ninasema ukweli, watu wanaweza kunilaumu lakini ninachoeleza ni ukweli. Wabunge wa CUF waliofukuzwa na chama hicho ni Severina Mwijage, Saumu Sakala, Salma Mwassa, Riziki Mngwali, Raisa Mussa, Miza Haji, Hadija Al-Qassmy na Halima Mohamed.
3
KOCHA wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema hajaridhishwa na maendeleo ya safu yake ya ulinzi baada ya kufungwa bao kwenye michezo minne mfululizo ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC). Akizungumza juzi kocha huyo alisema licha ya kufanikiwa kutinga kwenye hatua ya 16 bora ya Kombe la FA baada ya kuwang’oa Mwadui kwa mabao 2-1 kwenye mchezo ulichezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam bado anafikiria kuja na dawa itakayosaidia kuzuia hali hiyo.“Tumepata ushindi kwenye mchezo wa leo (juzi) na tumefanikiwa kusonga hatua inayofuata ni jambo nzuri kwa timu, lakini kwangu binafasi bado sijafurahishwa na safu yangu ya ulinzi katika michezo minne iliyopita kila mechi tumeruhusu kufungwa bao na kinachoniumiza kichwa zaidi ni namna wanavyofungwa, “ alisema Sven. Simba ukitoa mchezo dhidi ya Mwadui mechi zingine tatu ambazo Simba imefungwa licha ya ya kuibuka na ushindi ni pamoja na Alliance 4-1, mbele ya Mbao 2-1 na ule waliotaka sare ya kufungana mabao 2-2 dhidi ya Yanga. Alisema kinacho muumiza kichwa ni namna safu ya ulinzi inavyoruhusu kufungwa ni kutokana na kukosa mawasiliano na wakati mwingine wakishafungwa wanakuwa kwenye presha kubwa ya kutengeneza mazingira ya kutafuta bao la kusawazisha. Sven alisema kwenye mchezo huo kuanzia sehemu ya kiungo walicheza vizuri na kutengeneza nafasi nyingi za kupata mabao lakini kukosekana kwa umakini sehemu ya mwisho ilisababisha kuchukua muda mrefu hadi kufanikiwa kupata bao la ushindi kupitia Francis Kahata. Alisema ushindani walioupata kwenye mchezo ulipita ni maandalizi kuelekea kwenye mechi inayokuja ya ligi dhidi ya Coastal Union kuhakikisha wanaendeleza wimbi la ushindi kutengeneza mazingira ya kutetea ubingwa wa
4
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya,  alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele.  “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema
5
MLINDA mlango wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Juma Kaseja amefunguka kuwa kutokana na hamasa ya wachezaji iliyopo ndani ya timu hiyo kuna uhakika mkubwa wa kuibuka na ushindi katika mchezo dhidi ya Kenya.Tanzania na Kenya zinakutana leo Dar es Salaam kusaka tiketi ya kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (Chan 2020).Stars kwa sasa walipiga kambi na kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa Uwanja wa Boko Veterani, Bunju chini ya kocha mkuu Etiene Ndayiragije akisaidiana na Selemani Matola na Juma Mgunda.Akizungumza mara baada ya mazoezi, Kaseja ambaye pia ni mchezaji wa Klabu ya KMC alisema mchezo dhidi ya Kenya ni mgumu mno, lakini wanaamini watapata matokeo mazuri.Alisema kuwa kitu kinachomfanya aamini hivyo ni kutokana na ushindani mkubwa uliopo kwenye timu hiyo unaoneshwa kwenye mazoezi hali inayofanya kila mmoja kuweza kujiandaa ipasavyo na mchezo huo.Alisema kuwa mchezo wao dhidi ya Kenya ni mgumu lakini kutokana na kuwafahamu vizuri wapinzani wao na maandalizi mazuri waliyoyapata wana uhakika wa kushinda na kujitengenezea mazingira mazuri ya kukata tiketi ya mashindano hayo.“Kenya tumewahi kucheza nao mara nyingi, tunawafunga na wao wanatufunga kwakuwa wanakuja kucheza nyumbani hivyo tunauhakika wa kupata ushindi ili tujiwekee mazingira mazuiri katika mchezo uijao.“Hii ni timu ya taifa ya Tanzania kila Mtanzania ana haki ya kuitumikia, mazoezi ni mazuri tuliopo kikosini kila mmoja anapambana kupata nafasi ya kucheza, ushindani ukiwa mkubwa basi kuna uhakika wa kupata matokeo mazuri,” alisema Kaseja.
4
KILO 300 za mbegu za korosho zimekabidhiwa kwa wananchi kata ya Miyombweni wilayani Mbarali mkoani Mbeya kuzalisha miche 55,000 msimu ujao wa kilimo kwa kata hiyo pekee.Akikabidhi mbegu hizo jana, Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune aliwataka wakazi wilayani hapa kuchangamkia kilimo cha zao hilo kwa kupanda miche kwenye mashamba yao, maeneo ya mipaka na pia majumbani.Mfune alisema korosho ni kati ya mazao yenye faida kubwa kwa sasa kwa mtu mmoja mmoja, kwa serikali na inaweza kuwa chanzo kizuri cha kukuza makusanyo ya halmashauri ikitunzwa. Aliwataka wakazi wa Wilaya ya Mbarali kupanda zao la korosho kwenye mashamba yao na maeneo yao ya makazi kujiongezea kipato.“Mikorosho ni kama miti ya kawaida, mbegu zimekuja za kutosha, muangalie maeneo yaliyo wazi muoteshe na nyumbani pia”, alisema.Alisema, baada ya miaka mitano, mtakuwa watu wengine kwani hilo ni zao jipya, kila mmoja ajaribu kujielimisha awe mkulima bora. Diwani wa Kata ya Miyombeni, Mustaulo Sanzala alisema wananchi ambao hawaamini kuhusu korosho wanaweza kwenda kujionea kwa wakulima ambao miti ya o imeanza kutoa matunda, na baada ya miaka mitano wataamini kupitia mikorosho iliyopandwa kipindi hiki.Diwani huyo alisema katika kulipa uzito wa kipekee zao la korosho, baadhi ya vijiji katika kata yake kikiwemo Mapogoro wamethubutu kugawa mashamba kwa wananchi walioonesha nia ya kulima zao hilo ili wapande kwa wingi.Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbalari, Kivuma Msangi, Ofisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Wilaya, Daniel Kamwela alisema hadi sasa wakulima 229 wamesajiliwa kwa uzalishaji wa zao la korosho na hekta 328 zimepandwa zao hilo kwa wilaya yote tangu kuanza kutolewa kwa hamasa.Awali kabla ya mkutano na wananchi Mkuu wa Wilaya alitembelea baadhi ya mashamba ya mikorosho ya wakulima Kata ya Miyombweni kukagua vitalu vya kuoteshea mbegu hiyo.Mwaka 2018/2019 halmashauri iliweza kununua kilo 300 za mbegu za korosho kugawa kwa wakulima, na mwaka 2019/2020 halmashauri imeweza kununua kilo 500 za mbegu za korosho zinazotegemea kuzalisha miche 70,000.
3
0768670620 NA SHEILA KATIKULA-MWANZA UVUVI  haramu umeelezwa kuwa tatizo sugu  ndani ya Ziwa Victoria kutokana na vijana wengi  kutumia zana haramu katika shughuli hiyo, kitendo kinachosababisha samaki  wachanga na mazalia kuharibiwa. Kutokana na hali hiyo, Serikali imekuwa ikifanya operesheni ya kukamata nyavu na makokoro yasiyo na viwango na kuyateketeza bila kuwawezesha kupata vifaa bora ili kuendelea kuvua na kuinua uchumi wao. Kitendo cha Serikali kukamata bidhaa hizo haramu na kuziteketeza, kimekuwa kikilalamikiwa na wavuvi hao wakidai wao hawana makosa ispokuwa  wale wanaoziingiza nchini na kuziuza madukani, hivyo mara zote huomba Serikali ingefanya mpango wa kuzuiliwa mpaka bidhaa hizo ili zisiingie nchini. Pia wavuvi hao wamekuwa wakilalamika kwamba asilimia kubwa ya maduka yanayouza bidhaa hizo yanamilikiwa na viongozi wa Serikali, lakini wauzaji wakiwa ndugu zao na inafikia wakati baadhi ya bidhaa zinazokamatwa hurudishwa katika maduka hayo kwa njia  ya kinyemela. Binafsi naungana na Mkurugenzi wa Kambi ya  Fuata Nyao, Vedastus Msizu,  kwa kitendo cha kijitolea   kutoa zana  halali za  uvuvi  kwa zaidi ya vijana 12. Kiongozi ameamua  kutoa  vifaa vya uvuvi  Mitumbwi 14, injini  moja, nyavu 700 zenye thamani ya Sh  milioni  88.3 ambapo  zaidi ya vijana 45 watanufaika  na mpango huo  kwa kupata ajira. Zana  hizi zilizotolewa na mjasiriamali  huyu kwa lengo la  kusaidia  wavuvi  na   kupunguza  uvuvi haramu  ndani ya  ziwa hili, huku akisisitiza kuwa  kutolewa kwa  vifaa hivyo kutasaidia  samaki wadogo kubaki na mazalia  katika ziwa hilo. Jambo hili ni  la maana sana kwa wavuvi hawa kwani uvuvi haramu utapungua  na  hatimaye  samaki kuwa lukuki kama ilivyo kuwa hapo nyuma, kwani kwa sasa samaki wamebaki  kuwa historia  katika  ziwa hili. Uvuvi wa  kisasa una manufaa mengi   ikwemo kuokoa mazalia ya samaki  ambayo hayapo tayari kwa kitoweo na viumbe waliopo majini. Ili kuunga mkono mikakati ya  Rais Dk. John Magufuli  kwa kufufua uchumi wa viwanda, ni lazima kila mtu  kuwa na moyo wa kizalendo kwa  kufanya kazi kwa bidii na kulinda mali za nchi hii kwa kuvua samaki kwa kutumia zana halali. Ni jukumu  la  wadau na kampuni  nyingine  kuiga mfano huu wa kusaidia watu ambao wana kipato  cha chini  ili wajikwamue kiuchumi  na kukuza  uchumi wa  viwanda kwa kufanya kazi kwa bidii. Niungane na Mkurugenzi Vedastus  kwa  kuwataka wavuvi hao  kufuata sheria zilizopo kwa kutumia zana  halali  kwani wakienda kinyume na ahadi zao  watakuwa wamemtia doa  kwa sababu amejitoa katika kuwasaidia. Ikumbukwe  kuwa   Serikali imekuwa ikifanya operesheni katika ziwa hili kwa lengo la kukamata  na kukusanya  zana haramu ambazo zina madhara kwa  mazalia ya samaki  na kusahau  kuwawezesha ili kununua  zana bora  ambazo zina faida kwa ujumla na kuiondoa na uharamia. Kwenye  sherehe  hizo za  kukabidhi vifaa  hivyo  zilizohudhuriwa na viongozi kutoka  serikalini na  sekta binafsi, nilishuhudia  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John  Mongela, akitoa maagizo kwa  wananchi  kujitoa  katika  kufanya  kazi  sambamba na  kutoa    ahadi   kuwa  atakayetoa   taarifa za kweli kuhusu    watu   ambao  wanafanya vitendo vya  uhalifu, ujangili ziwani  Sh 10,0000  kama  zawadi ili kupunguza  uhalifu.
3
Na MWANDISHI WETU TIMU ya soka ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Queens’, jana ilifanikiwa kutinga fainali ya michuano ya Kombe la Afrika Mashariki na Kati (Cecafa Chalenji) kwa wanawake baada ya kuwachapa wenyeji Uganda mabao 4-1. Kilimanjaro Queens sasa itacheza mchezo wa fainali dhidi ya Kenya Jumanne, baada ya kuwafunga Ethiopia 3-2 katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali uliochezwa Uwanja wa Chuo cha Ufundi Njeru kilichopo mjini Jinja, Uganda. Katika mchezo wa jana, Kilimanjaro Queens ilianza kwa kishindo na kufunga mabao matatu kipindi cha kwanza, yaliyofungwa na Donosia Daniel dakika ya sita, Mwanahamisi Omari dakika ya 17 na Stumai Abdallah dakika ya 31. Hata hivyo, dakika chache baadaye, Asha Rashid aliipatia Kilimanjaro Queens bao la nne kabla ya Uganda kupata bao la kufutia machozi. Kilimanjaro Queens iliyokuwa imepangwa Kundi B kwenye michuano hiyo, ilianza kwa kuichapa Rwanda mabao 3-2 kabla ya kutoka sare ya kutofungana na Ethiopia. Wawakilishi wengine wa Tanzania kwenye michuano hiyo ni timu ya taifa ya Zanzibar iliyokuwa imepangwa Kundi A, iliondoshwa kwa aibu baada ya kufungwa jumla ya mabao 30-1 katika michezo mitatu waliyocheza.
4
Bethsheba Wambura Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema nchi yake itaendelea kuimarisha uhusiano na Tanzania bila kujali maneno ya wanasiasa yanayotaka kuuvuruga. Kenyatta ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Julai 5, wakati akihutubia wananchi na viongozi waliojitokeza kumlaki alipotua katika Uwanja wa Ndege Chato mkoani Geita kwa ziara ya siku mbili hapa nchini. “Tuko hapa kuimarisha urafiki na tupo na wananchi wanaojuana na wanaozungumza lugha moja ya kinyumbani na kitaifa, ufike Namanga ni majirani kwa lugha ya nyumbani na kitaifa, upande wa Pwani hadi Taveta ni jamii moja, mtu anawezaje kututenganisha. “Haiwezekani siasa tuanze nayo kila wakati ukinywa chai siasa, ukienda ‘lunch’ siasa ukienda kwa mpenzi wako ni siasa haiwezekani kila siku ni siasa ina wakati, tujipange kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu mambo hayo ndiyo yatabadilisha maisha,” amesema Rais Kenyatta. Aidha, Rais Kenyatta amesema hata michezo inaimarisha ujirani kati ya nchi hizo mbili huku akikumbushia mechi kati ya Timu ya Taifa Stars na Harambee Stars zilipomenyana katika fainali za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon), zinazochezwa nchini Misri ambapo Harambee ilishinda 3-2. “Juzi tumechapana kule Cairo kila mtu na timu yake huku Harambee Stars huku Taifa Stars, sidhani kama kuna mtu alilala siku ile ila ndiyo hali ya mpira safari hii Kenya imeifunga Tanzania lakini hata ninyi mlifaidika tulipocheza na Senegal, nyinyi mlifungwa mbili na sisi tulifungwa tatu,” amesema.
3
MFANYABIASHARA maarufu mkoani hapa, Hans Paul amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani hapa kwa kosa la kuajiri raia watatu wa kigeni bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi nchini.Mfanyabiashara huyo anamiliki kampuni tatu jijini hapa ambazo ni Dharam Singh Hans Paul & Sons LTD, Hans Paul Ltd na Hans Paul Automech. Washtakiwa waliofikishwa mahakamani hapo ni Kumar Vemula (27) raia wa nchini India, Vinoth Krishanth (29) raia wa Sri Lankan na Raiph Leopold Hruscka (54) ambaye uraia wake haukutajwa.Wakisomewa mashtaka hayo na Wakili wa Serikali, Khalili Nuda mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Niku Mwakatobe, ilidaiwa kuwa mtuhumiwa wa kwanza, Hans Paul Novemba 12, mwaka huu alikamatwa akiwa ameajiri raia hao wa kigeni bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi nchini, huku akijua kuwa ni kinyume cha sheria.Watuhumiwa wengine Krishanth, Hruscka na Vemula kwa pamoja wanashtakiwa kwa kosa la kufanya kazi nchini bila ya kuwa na vibali. Vemula na Hruscka walikuwa wanafanya kazi kwenye kampuni ya Hans Paul Automech kama wahandisi washauri wa kiwanda hicho ambapo Krishanth anafanya kama mhandisi wa magari.Baada ya kusomewa mashtaka hayo, watuhumiwa wote kwa pamoja walikiri makosa yao ambapo Wakili wa Serikali aliiomba mahakama muda wa kuandaa maelezo ya awali ili waweze kusomewa kwa ajili ya hukumu.Kutokana na maombi ya Wakili wa Serikali Niku aliieleza mahakama hiyo kuwa dhamana za watuhumiwa zipo wazi na kuwataka kuwa na wadhamini wawili wenye vitambulisho pamoja na fedha kiasi cha Sh milioni tano kila mmoja. Baada ya kuwaeleza watuhumiwa masharti hayo, wakili wa utetezi aliyefahamika kwa jina moja la Ngereka aliiomba mahakama hiyo kuwa wateja wake hawana wadhamini na kuomba muda kwa ajili ya kuwatafutia wadhamini hao.Maombi hayo yalikubaliwa na Hakimu Niku ambaye alisema kuwa watuhumiwa wataendelea kukaa rumande mpaka watakapokidhi masharti ya dhamana. Watuhumiwa hao walirudishwa rumande lakini baada ya saa chache walikidhi vigezo vya dhamana na kesi hiyo kuahirishwa hadi Desemba 6, mwaka huu. Awali watuhumiwa hao walitiwa mbaroni Novemba 12, mwaka mwaka huu na Kamishna wa Kazi nchini Gabriel Malata alipofanya ziara katika kiwanda hicho.
3
KOCHA wa mabingwa wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Simba, Masoud Djuma amesema timu anayotaka msimu ujao ni kila mmoja awe na uwezo wa kugombea nafasi kwenye kikosi cha kwanza.Akizungumza na gazeti hili jana, Djuma alisema ligi ijayo huenda ikawa ngumu kwa sababu watakuwa na Simba tofauti kwani wanadhamiria kuwatengeneza wachezaji ili kila mmoja aoneshe ubora wake.“Tutakuwa na Simba ambayo kila mtu atatamani kucheza na kuonesha kiwango, mabadiliko makubwa yanakuja tukijua wazi ugumu wa ligi inayokuja, tunahitaji kila mmoja atambue wajibu wake kwa kucheza kwa kiwango,” alisema.Djuma alisema wanahitaji kuwa na wachezaji wenye uwezo ili watakapomtoa mtu na kumuingiza mwingine isiwe tabu waendeleze ushindani.“Hatutaki ukimtoa mchezaji mmoja unaanza kuwaza uwezo wa mwingine, kila mmoja akiwa mwenye ubora hupati tabu, unatoa kiwango na kuingiza kiwango, ushindani ni muhimu,” alisema.Kwa upande wake, Kaimu Rais wa klabu hiyo Salum Abdallah ‘Try again’ aliwataka mashabiki wa timu hiyo kuwapa nafasi kwani wamedhamiria kutengeneza kikosi chenye ushindani wa hali ya juu kwa ajili ya msimu ujao.Alisema, wekundu hao watakuwa kwenye maandalizi ya wiki tatu kujiandaa na Wiki ya Simba na michuano ya ligi mwezi ujao. Huenda wakaenda Uturuki Ijumaa ya wiki. “Wanachama na mashabiki wetu watulie na kutupa nafasi wakati tunatengeneza timu, tumeshasajili baadhi na tunaendelea kuboresha ili kuwa na kikosi bora chenye ushindani,” alisema.Simba imemaliza ya pili michuano ya Kagame iliyomalizika wiki iliyopita baada ya kufungwa mabao 2-1 na Azam hivi karibuni ilishika nafasi ya pili kwenye michuano ya Kombe la Kagame baada ya kufungwa 2-1 na Azam FC katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
4
MTENDAJI Mkuu wa timu ya soka ya Arusha United (CEOI), Elias Fikiri na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Fred Minziro 'Baba Ubaya' wametupiwa virago na uongozi wa timu hiyo baada ya timu hiyo kuwa na mwenendo mbovu katika Ligi Daraja la Kwanza inayoendelea.Kutimuliwa kwa Kocha na Ceo kumethibitishwa na viongozi wa timu hiyo na tayari waliochukuwa nafasi hizo wameshaanza kazi ya kuisaidia timu hiyo kufanya vizuri katika Ligi Daraja la Kwanza na hadi kupanda Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.Nafasi ya CEO wa Arusha United imechukuliwa na Otte Ndaweka  na Kocha Mkuu wa timu hiyo ameteliwa kocha mwenye daraja la kwanza, Hemed Moroco.Minziro amekiri kutimuliwa katika timu ya Arusha United kwa madai ya timu kushuka kiwango na kusema kuwa hana pingamizi na madai ya viongozi wa timu hiyo kwa sababu wameyatoa wao.Minziro amesema, anachokisubiri ni stahiki zake ya kuvunjwa kwa mkataba na ana imani atalipwa kilichochake bila ya kusumbuana.‘’Ni kweli nimetimuliwa na uongozi wa Arusha United na sasa ninasubiri haki yangu sina mengi ya kuzungumza mengine waulize wao wenyewe,’’amesema Minziro.CEO aliyetumiliwa katika timu hiyo, Fikiri amesema, hajatimuliwa bali amepisha upepo mkali uliopo katika timu hiyo, ambao ameona hawezi kasi yake.Fikiri alisema kama viongozi wa Arusha United wamesema yeye ametimuliwa hawezi kuwazuia kusema hilo lakini yeye ana amini kuwa hajatimuliwa bali ameamuwa kujiengua mwenyewe kwa hiari yake.''Sijatimuliwa ila niliondoka mwenyewe kwa hiari yangu kuiongoza timu hiyo na kama wao wamesema wametimuwa wabarikiwe,'' alisema Fikiri.Baada ya kuteuliwa kuwa CEO mpya wa Arusha United, Ndaweka amekiri kushika nafasi hiyo na kuomba ushirikiano kwa wadau wote wa soka mkoani Arusha lengo likiwa kuhakikisha timu hiyo inafanya vema katika Ligi Daraja la Kwanza na hatimaye timu hiyo kupanda Ligi Kuu.‘’Ni Kweli nimeteuliwa kuwa Ceo wa Arusha United na ninachoomba ushirikiano kutoka kwa wadau wa soka, lengo ni kutaka timu hiyo kupanda daraja.’’‘’Tufungue ukurasa mpya yaliyopita yamepita kwa sasa tusonge mbele lengo ni kutaka Arusha United icheze Ligi Kuu na kikubwa ni ushirikiano na sio vinginevyo,’’ amesema Ndaweka.Kocha Morocco amesema, bado hajapata taarifa rasmi za kuifundisha timu hiyo, lakini amekuwa akizisikia mitaani, ambapo yuko tayari kuifundisha timu hiyo endapo itakuwa kweli.Iwapo Morocco atakubaliana na uongozi wa Arusha United atasaidiana na kocha Juma Masoud na meneja wa vifaa Khatibu Ally maarufu kwa jina la Bambucha.
4
Mwandishi Wetu -Singida BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 katika wilaya kadhaa nchini. Misaada iliyotolewa na benki hiyo inayoongoza kwa kutengeneza faida kati ya benki zote zinazofanya biashara humu nchini ndani ya miezi mitano mwaka huu, inahusisha vifaa vya ujenzi, madawati na vifaa vingine vinavyowezesha ukamilishaji wa miradi ya afya,elimu na usalama wa raia. Benki  ya NMB imeshatoa  msaada wa  vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa mikoa ya Kanda ya Kati. Akifafanua kuhusu misaada hiyo wakati akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani ingida, Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi, alibainisha kuwa misaada hiyo ya zaidi ya Sh milioni 200 iliyotolewa imelenga sekta ya elimu, afya  na majanga kwa mikoa mitatu ya  Kanda ya kati. Akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, MkoaniSingida, katika shule ya Sekondari ya New Kiomboi, Mlozi alisema fedha hizo zilizotolewa na NMB zimetumika kununua madawati, viti vya shule za sekondari,vitanda na vifaa tiba kwenye sekta ya afya. Aidha, alisema lengo la misaada hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali. Pia alisema misaada hiyo imekabidhiwa kwa baadhi ya shule, zahanati, hospitali katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Pia NMB walikabidhi madawati 250 na vitanda 80 vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 29.5 kwa baadhi ya shule za Wilaya ya Iramba mkoani humo. Katika hatua nyingine, Benki hiyo imevipatia kituo cha Polisi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro pamoja na shule ya msingi Msowelo mabati 160 yenye thamani ya Sh5 milioni kwa ajili ya kuezekea maboma. NMB iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni mpango wa kuzipunguza baadhi ya changamoto kwa taasisi za serikali hapa nchini, Meneja wa NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus, alisema na kubainisha kuwa msaada huo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ili kusaidia kuinua miradi ya maendeleo. Baraka alisema kuwa kati ya mabati hayo, kituo cha polisi wilaya kimepa tamabati 80 huku shule ya msingi Msowelo nayo ikipata mabati 80.
5
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM BENKI ya I&M Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, lakini inang’ara kwa kutoa bidhaa na huduma za kipekee ambazo zinakidhi mahitaji yote ya mteja katika soko. I&M Tanzania ilitambulisha akaunti mpya ya wanawake ya Tunaweza inayotoa suluhisho kwa wanawake wa ngazi zote kuanzia mmoja mmoja, wajasiriamali hadi kikundi au taasisi. Akaunti hiyo inajitofautisha kwa kutoa huduma bila malipo yoyote, haina makato ya kila mwezi na viwango vyake vya riba vinavutia kwenye akiba. Akizungumza leo jijini Dar es Salaa, katika maonyesho hayo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo, alisema kuwa bidhaa hiyo mpya imeunganishwa kwenye mtandao wa benki wa kidijitali ili kuwapa wateja huduma bora na endelevu wakati wowote wanapohitaji. Alisema I&M Tanzania ni sehemu ya I&M Holdings Kenya iliyoanzishwa mwaka 1974 kama kampuni ya huduma za kifedha kabla baadaye kubadilishwa kuwa benki ya biashara. “Mwaka huu inasherehekea miaka kumi ya huduma zetu katika soko la Tanzania. Tunafurahi kuendelea kuhudumia wateja wetu na wateja wapya, pia tunashukuru wateja wetu na washikadau wote walioshiriki katikakuiletea benki mafanikio makubwa kwa kipindi chote cha miaka kumi kwenye soko.” “Tunatoa huduma kadhaa za kifedha ikiwa ni pamoja na akaunti ya akiba, current akaunti kwa madhumuni ya biashara, mikopo ya biashara, huduma za kubadili fedha, uhamishaji fedha kitaifa na kimataifa, huduma za kidijitali ambazo hutoa fursa kwa mteja kupata huduma za benki kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *150*32# au kupitia iClick- huduma ya benki kwa njia ya mtandao inayopatikana bila kikomo kwa saa 24,” alisema Anitha Meneja Masoko na Mawasiliano huyo wa benki hiyo, alisema kuwa pia benki yao wanatoa unafuu na urahisi wa kupata mikopo na huduma nyingine kadhaa ambazo ziliwafanya watu waliotembelea banda lake kwenye maonyesho ya Sabasaba lililopo ukumbi wa Karume, upande wa kulia wa lango la kuingilia kuhamasika na kutaka kujua zaidi kuhusu benki hiyo. “I&M inafungua milango kwa Watanzania wote kwenda kujiunga na benki inayojali mahitaji yao, iliyo tayari kuwapa huduma za kipekee za kifedha kupitia wafanyakazi wake wenye uzoefu zaidi katika kutoa huduma bora kwa wateja. “Mbali na kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba, benki hiyo inatoa huduma zake bora kupitia mtandao wa matawi yake yaliyoko maeneo ya Maktaba, Indira Gandhi, Nyerere, Kariakoo, Oysterbay pamoja na mikoani ikiwa ni pamoja na Moshi, Arusha na Mwanza,” alisema Timu ya wafanyakazi wa mauzo na idara ya masoko wa benki hiyo kutoka matawi yake ya Dar es Salaam inayoongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wapo kwenye maonyesho hayo ili kuwapa wageni na wale ambao wanataka kuwekeza katika benki inayoaminika na salama ikiwa na huduma za ATM zinazopatikana kwa saa 24.
5
ROBERTO Oliveira amewapongeza wachezaji wake wa Rayon Sports baada ya kuifunga Kirehe mabao 4-0 na kutwaa taji la Ligi Kuu ya Rwanda ya Azam msimu wa mwaka 2018-19.Rayon Sports ambayo imeivua ubingwa APR, imetwaa taji hilo huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi kabla ya kumalizika kwa ligi hiyo inayoshirikisha timu 16. Hilo ni taji la kwanza kwa klabu hiyo tangu mwaka 2017, na ni la tatu katika kipindi cha miaka sita iliyopita. Mchezaji anayepewa nafasi kubwa ya kuibuka na kiatu cha dhahabu, Jules Ulimwengu na mshambuliaji mzaliwa wa Ghana, Michael Sarpong wote walizifumania nyavu na kuizamisha kabisa timu hiyo iliyokuwa katika hatari ya kushua daraja katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Nyakarambi.Rayon Sports, ambayo pia inajulikana kama the Blues, watakabidhiwa taji lao Juni Mosi wakati watakapokuwa wenyenyeji wa Marines katika mchezo wao wa mwisho utakaopigwa kwenye Uwanja wa Kigali. “Nimefurahia sana kushinda taji langu kubwa nikiwa na Rayon Sports. Hili ni jambo la kuhistoria,” alisema Roberto alipozungumza na Sunday Sport.“Licha ya kuanza kwa kusuasua, timu nzima imecheza vizuri msimu mzima. Tulikuwa na kampeni kabambe ya ligi, hasa katika nusu ya pili.” Kocha huyo Mbrazili alisema sifa kubwa wanastahili kutokana na timu kutekeleza majukumu yake vizuri kila aliyekuwa na uhusiano mzuri katika klabu kuanzia klabu na benchi lote la ufundi pamoja na mashabiki wetu. “Bado nahisi kama ni ndoto, kile kilichotokea katika msimu,” aliongeza. “Ninachoweza kusema ni shukrani kwa wachezaji wangu, kwani wameonesha kiwango kikubwa bila ya kukata tamaa.”MABINGWA APRMabingwa wa zamani APR mwishoni mwa wiki walijikuta wakipokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Espoir, ikiwa ni wiki moja baada ya kupoteza mchezo dhidi ya AS Muhanga iliyokuwa pungufu na wachezaji 10.APR ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Muhadjiri Hakizimana katika dakika ya 62 katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Kigali, lakini furaha yao ilizimwa na Fred Kyambadde dakika 10 baadae kabla Sadi Nkundimana hajafunga la ushindi katika dakika za majeruhi na kuwapatia ushindi wageni.Timu hiyo ya Jeshi la Rwanda, ambayo inatakiwa kushinda Kombe la Amani 2019 kama wanataka kushiriki mashindano ya Afria msimu ujao, imeshinda mara mbili tu katika mechi zake nane zilizopita. Huku ikiwa imebaki mechi moja kabla ya kukamilika kwa msimu wa ligi, APR iliyopo katika nafasi ya pili wamepitwa na mabingwa Rayon kwa pointi saba.
4
AGATHA CHARLES NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM VIONGOZI wawili, aliyekuwa Katibu wa Kwanza wa Rais (Ikulu- Habari ) wa Rais wa Awamu ya Kwanza, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Paul Sozigwa (84) na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu, wamefariki dunia jana, nyakati tofauti wakiwa wanapatiwa matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma wa Taasisi hiyo, Anna Nkinda, alisema Sozigwa alifariki usiku wa kuamkia jana. “Tulimpokea marehemu Aprili 25, mwaka huu akitokea wodi ya Mwaisela ambako alikuwa amelazwa, na kuanza kumpatia matibabu dhidi ya ugonjwa uliokuwa unamsumbua, Mei 9, mwaka huu afya yake ilianza kuimarika na akatolewa katika wodi ya uangalizi maalumu na kuhamishiwa katika wodi namba mbili,” alisema. Nkinda alisema huko aliendelea kupatiwa matibabu na daktari wake hadi usiku wa kuamkia jana saa mbili na nusu ambapo alifariki dunia. Naye, mtoto wa marehemu, Lucy Sozigwa, alisema msiba upo eneo la Mtoni, jirani na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) ambako ni nyumbani kwa mtoto wake mkubwa, Mchungaji Moses Sozigwa. “Msiba uko hapa nyumbani kwa kaka Mchungaji Moses, Mungu akipenda tunatarajia kuzika siku ya Jumatatu huko Kisarawe, mkoani Pwani,” alisema Lucy. Lucy alipotakiwa kueleza marehemu Sozigwa alikuwa akisumbuliwa na nini, alisema, kaka yake (mtoto wa marehemu pia) Moses ndiye angeweza kueleza kwa kina chanzo hicho. Alipotafutwa Mchungaji Moses alisema baba yao alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kupoteza kumbukumbu kwa muda mrefu. “Mzee alikuwa mtu mzima, na katika umri huo tunaelewa kichwa kinakuwa kimechoka, na hali hiyo ilisababisha pia kupata tatizo lingine la moyo na uvimbe,” alisema. Alisema jambo ambalo akilikumbuka linamuumiza kutokana na kifo cha baba yake, ni ule uzalendo aliokuwa nao kwa nchi yake. “Alikuwa mzalendo wa kweli, sasa hivi tunaona uzalendo unapungua, baba aliipenda nchi, alifanya kazi kwa bidii siku zote, nikikumbuka jambo hilo naumia mno,” alisema. Marehemu Sozigwa atakumbukwa kwa kushika nyadhifa mbalimbali nchini kabla ya kustaafu utumishi serikalini mwaka 1983. Nyadhifa hizo ni pamoja na mwaka 1967 aliteuliwa kuwa Katibu wa Kwanza wa Rais (Ikulu-Habari ), Mkurugenzi Mkuu wa Kwanza wa Redio Tanzania (RTD), Ofisa Wilaya (DO), Wilaya ya Kisaraswe katika Serikali ya Kikoloni na Katibu Mkuu, Wizara ya Habari na Utangazaji. Mbali na hizo, pia amewahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ikiwamo kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Kamati Kuu (CC) na Mwenyekiti wa Idara ya Udhibiti na Nidhamu na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani. Katika salamu za rambirambi, CCM kupitia Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole, kilisema pamoja na kupokea taarifa hizo kwa mshituko, kitamkumbuka na kumuenzi marehemu Sozigwa kama mmoja wa waasisi wa Taifa na chama hicho. Polepole katika taarifa yake alisema marehemu Sozigwa alihudumu katika uongozi wa kabla na baada ya Uhuru wa Tanzania Bara (Tanganyika) na baadaye Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. “Jambo mojawapo ambalo ameshughulika nalo tangu awali ni uimarishaji wa misingi ya maadili na miiko ya uongozi CCM, kipekee sana ametumika kama Mtendaji Mkuu wa iliyojulikana kama Idara ya Udhibiti na Nidhamu ambayo sasa inajulikana kama Kamati ya CCM ya Usalama na Maadili, Uongozi chini ya Mwenyekiti John Magufuli,” alisema Polepole. Polepole alisema, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, pia alitoa pole kwa familia, akisema utumishi na uongozi wa marehemu Sozigwa katika maadili na miiko ya uongozi unaendelea kuwa chachu ya kutenda siasa safi na uongozi bora ndani ya chama. Katika mitandao ya kijamii kumekuwa na watu mbalimbali wanaomwelezea marehemu Sozigwa kuwa alikuwa na sifa kuu inayompambanua kuwa katika maisha yake yote ya siasa alihubiri kile alichokiamini. Moja ya vipindi anavyodaiwa kuvianzisha akiwa Redio Tanzania ni ‘Mikingamo’ pamoja na kupinga ubepari huku akidaiwa aliishi kijamaa. Akizungumzia kifo cha Mwambungu, Nkinda alisema naye alifariki dunia jana akiwa JKCI alikokuwa amelazwa kwa matibabu dhidi ya ugonjwa uliokuwa ukimsumbua. “Mwambungu aliletwa JKCI Mei 10, mwaka huu akitokea Emergence (Idara ya Magonjwa ya Dharura), alipelekwa wodi ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu kwa matibabu, ambako alifariki dunia,” alisema Nkinda. Itakumbukwa kuwa Mwambungu alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma tangu mwaka 2011, enzi za utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kikwete na hata Rais Dk. John Magufuli alipoingia madarakani aliendelea naye. Marehemu Mwambungu aliondolewa katika mabadiliko yaliyofanywa na Rais Magufuli Juni, 2016 na kurudishwa kuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Dar es Salaam, ili kupangiwa kazi nyingine. Rais Dk. John Magufuli jana alizitumia salamu za rambirambi familia za marehemu Sozigwa na Mwambungu. Kupitia taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa, Rais alisema Marehemu Sozigwa atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, uchapakazi na uadilifu. “Natambua kuwa marehemu Sozigwa ni miongoni mwa waasisi wa Taifa letu ambao walijitoa kwa dhati kupigania nchi yetu kabla na baada ya Uhuru. Alishirikiana na waasisi wengine, akiwamo Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizolikabili Taifa baada ya uhuru, zikiwamo kupiga vita ujinga na maradhi ndani ya chama na serikali, hakika tutazienzi juhudi zake,” alisema Rais Magufuli. Kuhusu marehemu Mwambungu, Rais alisema alikuwa ni kiongozi wa aina yake, moyo wake na upendo ulimwezesha kufanikiwa katika kazi zake, na alipigania maendeleo ya wananchi pamoja na kutatua jambo kwa njia ya mazungumzo.  
3
STRASBOURG, UFARANSA BUNGE la Ulaya jana lilitarajia kuijadili Kenya, siku chache tu baada ya jopo lake la waangalizi wa uchaguzi kuchapisha ripoti iliyounanga uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo mwaka jana. Bunge linakutana mjini hapa na mjadala kuhusu Kenya ulitarajia kuanza jana saa 11 jioni za Afrika Mashariki. Mkuu wa jopo hilo, Marietje Schaake, ni miongoni mwa waliotarajia kuhudhuria majadiliano hayo. Schaake aliweka ujumbe wake katika akaunti yake ya Twitter juzi jioni akisema: “Kesho mchana Bunge la Ulaya litafanya mdahalo kuhusu hali ya nchini Kenya. Nitatoa taarifa kwa muhtasari wakati matokeo ya mjadala yatakapofahamika.” Wiki iliyopita, Schaake alitupiana maneno na Serikali ya Kenya baada ya kutoa ripoti ya jopo lake mjini Brussels, Ubelgiji badala ya Kenya, ambako anasema yeye na jopo lake hawakutakiwa. Wakati akidai kuwa Serikali ya Kenya haikuwa tayari kulipokea jopo hilo, Kenya ilisema kutoa ripoti bila kuishirikisha ni makosa na dharau. Lakini Schaake alisema wakati makubaliano ya tarehe za utoaji ripoti yaliyofikiwa Juni mwaka jana zikikaribia, Serikali haikuonyesha utayari wa kuwapokea na hivyo kuamua kuitoa kwingine. Balozi wa Kenya nchini Ubelgiji, Johnson Weru, alisema ni Schaake aliyeenda kinyume cha makubaliano. Rais Uhuru Kenyatta alishinda uchaguzi wa marudio na kutetea urais kwa muhula wa pili baada ya ushindi wake wa awali kufutiliwa mbali na Mahakama ya Juu. Lakini jopo la waangalizi lilisema Wakenya walikuwa na matumaini makubwa, ambayo hata hivyo yaligeuka kuwa ya kufadhaisha na kuliacha taifa likiwa limegawanyika. Ripoti hiyo imesema kuwa mchakato wa upigaji kura uliharibiwa na hatua ya viongozi kuzishambulia taasisi huru na kutofanyika kwa mazungumzo baina ya pande mbili hasimu, jambo lililochangia kuenea mizozo na machafuko.
2
MKUU wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela ameomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kusaidia uzalishaji wa mitamba 1,000 kwa ubia na sekta binafsi (PPP) ili kuwezesha kuwepo mpango mkakati wa kuinua zao la maziwa mkoani humo.Pia aliomba wizara kusaidia upatikanaji wa madume bora ya asili ya Bomani na Sahiwah ya India, Gir na Cerrralando kutoka Brazil ambayo huboresha sana uzalishaji wa maziwa na nyama.Katika taarifa ya Mkoa wa Tanga ya Maendeleo ya Mifugo aliyoisoma kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega mwishoni mwa wiki, Shigela amesema mkakati huo unatokana na upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga (Tanga Fresh) kuongeza uwezo wa kuzalisha baada ya kupata mkopo Sh bilioni 12.Alisema mkopo huo umeleta manufaa kwa kuongeza uwezo wa kuzalisha maziwa ya muda mrefu kutoka lita 50 hadi 120 kwa siku huku upatikanaji malighafi hiyo ukiwa pungufu kwa lita 70, jambo linalohitaji mkakati mzuri wa kuongeza uzalishaji wa maziwa hayo.Shigela alisema mafanikio hayo yameongeza pia ukubwa wa uhitaji wa malighafi ambapo uzalishaji mdogo wa maziwa wa lita 70 kwa siku umeshindwa kukidhi mahitaji ya kiwanda ya lita 120 na kuwa changamoto nyingine.Alisema kama mkoa na wizara zikishirikiana na taasisi za kiserikali Tanga na mashamba ya nje ya mkoa, changamoto hiyo inaweza kumalizika.Kuhusu upigaji chapa mifugo alisema ng’ombe na punda 536,533 walipigwa chapa kama lengo la upigaji chapa 503,545 sawa na asilimia 106.6 ya mifugo yote ya Mkoa wa Tanga lilivyokuwa.Shigela alisema changamoto hiyo imetokana na wafugaji wengi kutofuga kibiashara hivyo kushindwa kumudu bei za pembejeo na huduma za mifugo na tija ndogo ya uzalishaji kutokana na mifugo na mifumo ya uzalishaji mifugo.Alitaja changamoto nyingine kuwa ni upungufu wa wagani ulio asilimia 50 hasa vijijini na uhaba wa nyenzo, malisho na maji hasa kiangazi.Ulega aliahidi kushirikiana na mkoa ili kero zilizoainishwa kwenye taarifa hiyo zinapatiwa ufumbuzi ili kukiwezesha kiwanda hicho kufikia lengo na kuwa mkombozi kwa wafugaji.
3
SERIKALI imesema uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ya kuzuia Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri (DEDs) kusimamia uchaguzi, hayawezi kuathiri uchaguzi wowote wa marudio wala uchaguzi zijazo.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi (pichani) alisema tayari wametoa taarifa ya nia ya kukata rufaa Mahakama ya Rufani ya Tanzania kupinga uamuzi uliotolewa Ijumaa iliyopita na jopo la majaji watatu.Amesema amekuwa akiulizwa kuhusu athari za uamuzi huo kuhusu uchaguzi ujao na chaguzi ndogo za marudio hivyo hawapaswi kuwa na wasiwasi kwani nafasi ya kukata rufaa ipo.Profesa Kilangi amesema, mpaka sasa hawajapata nakala ya uamuzi huo ili waweze kujiridhisha ni kitu gani hasa mahakama hiyo imeelekeza. Pia alisema kuwa kwa misingi ya sheria pale serikali inapotoa taarifa ya kukata rufaa kwenda Mahakama ya Rufani, inaifanya hukumu hiyo isitekelezeke.“Kwa mujibu wa kifungu cha 14 (3) cha Sheria ya Utekelezaji wa haki na wajibu inasema serikali kwa maana ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia kwa Wakili Mkuu wa Serikali akishatoa taarifa ya nia ya kukata rufaa basi hiyo taarifa moja kwa moja inazuia utekelezaji wa hukumu ile,” alifafanua Profesa Kilangi.Alisisitiza kuwa ibara ya 30 (5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeeleza mambo yanayoweza kufanyika katika mazingira kama haya na katika sheria kifungu cha 13 pia kimeeleza.Akizungumzia sababu za kukata rufaa, Profesa Kilangi alisema wanakata rufaa kupinga ubatilishwaji wa kifungu cha 7 (1) na kifungu cha 7(3) ambavyo mahakama ilisema kuwa vinakinzana na Katiba ya mwaka 1977.Katika vifungu hivyo vya sheria ya uchaguzi ambavyo vinatamka kuwa Mkurugenzi wa Jiji, Manispaa na Halmashauri anaweza kusimamia uchaguzi na kifungu cha 7(3) kinaipa mamlaka Tume ya Uchaguzi kuteua wasimamizi wa uchaguzi miongoni mwa watumishi wa umma pale inapoona inafaa.Alisema kuwa baadhi ya vifungu ambavyo mwanachama wa Chadema, Bob Wangwe alivipinga mahakamani iliona havina ukinzani na badala yake ni halali kuendelea kutumika kama vile kifungu cha 6 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ambacho kinamtambua Mkurugenzi wa Uchaguzi anateuliwa na Rais kutoka katika utumishi wa umma na kifungu cha 7 (2).
3
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
5
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019  kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na  kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi  kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na  kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza.  “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake.
5
WATOTO 150 nchini wamefanyiwa upasuaji wa moyo ambapo kati yao 95 wamefanyiwa upasuaji kwa njia ya kufungua kifua huku 60 wakifanyiwa bila ya kufunguliwa vifua katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dar es Salaam.Upasuaji huu umefanyika katika kipindi cha kati ya Januari hadi Oktoba, mwaka huu. Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji, sasa taasisi hiyo inajenga wodi maalum itakayokuwa ikilaza watoto peke yao tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo watoto wanalazwa wodi moja na watu wazima.Baada ya mradi huo kukamilika, wodi itakuwa na vitanda 32 ambapo nane vya watoto wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) na 24 katika wodi za kawaida. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo Alhamisi, baada ya kupokea msaada wa Sh milioni 20 kutokea kampuni ya Tatu Mzuka, Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Profesa Mohamed Janabi amesema kuna ongezeko la watoto wanaozaliwa na magonjwa ya moyo nchini.Akielezea kwa takwimu, Mkurugenzi huyo amesema zaidi ya asilimia 75 ya watoto wanaofanyiwa upasuaji hospitalini hapo wana matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo, akiyataja kuwa ni matundu na magonjwa yanayoshambulia milango ya mishipa mikubwa na midogo ya moyo.Ameongeza kuwa asilimia 25 ni wale watoto waliopata matatizo hayo baada ya kuzaliwa ambapo alisema asilimia hiyo imekuwa ikishuka. Kwa upande wake Mkuu wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Sebastian Maganga alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya kampuni hiyo kuisaidia jamii na kuahidi kuendelea kuisaidia zaidi hospitali hiyo.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesisitiza utawala bora katika utoaji wa huduma za kibenki. Ameeleza kuwa mwaka jana serikali ilifungia benki tano zilizofilisika na kusababisha hasara kwa wanahisa pamoja na wananchi waliofungua akaunti katika mabenki hayo, kutokana na ukosefu wa utawala bora na tamaa kwa watumishi.Pia, amesema kuwa serikali inaratibu vyema mfumo wa utoaji wa fedha za kigeni, kwa kuanza na mabenki mbalimbali na baadaye Benki Kuu (BoT) itaweka utaratibu wa kufungua maduka mengine ya kigeni ya kimkakati katika maeneo mbalimbali nchini.Akifungua semina ya wanahisa wa Benki ya CRDB jana Jijini Arusha, Waziri Mkuu Majaliwa alisema hivi sasa BoT inakamilisha utaratibu wa kufungua maduka ya kubadilisha fedha ya kimkakati ili kuwezesha maduka ya kubadilisha fedha za kigeni yaliyofungwa awali, kufanya kazi katika maeneo ya kimkakati.Aliwaondoa hofu wafanyabishara wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni na kuwataka kutokuwa na wasiwasi kwani Benki Kuu ya Tanzania, mara itakapokamilisha taratibu zake, maduka hayo yatafunguliwa kwa utaratibu utakaowekwa Alisisitiza pia utawala bora ni muhimu kuzingatiwa na kuitaka Benki ya CRDB itoe elimu ya mjasiriamali ili waweze kujua matumizi ya fedha zao, ikiwemo elimu ya mjasiriamali ili wananchi waepukane na uuzwaji wa nyumba zao au mali walizonazo.“Sitegemei benki hii kufilisika bali itakuwa mfano kwa mabenki bora yanayozingatia utawala bora, pia wale waoliofungiwa kufanya biashara za kubadilisha fedha katika maduka mbalimbali nchini, wasubiri Benki Kuu inafanya utaratibu na ikikamilisha yatafunguliwa maduka ya kimkakati katika maeneo mbalimbali nchini,” alisema.Waziri Mkuu alisisitiza kuwa serikali inatambua mchango wa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRBD, Dk Charles Kimei na kumtaka mkurugenzi wa sasa kuhakikisha anafuata nyayo zake ili aweze kuhakikisha benki hiyo inakua kwa kasi, ikiwemo kutoa elimu ya kieletroniki kwa wananchi ili kuendana na kasi ya kiteknolojia Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema benki hiyo imeweka vipaumbele vitano, ikiwemo uboreshaji wa huduma kwa wateja, kuongeza matumizi ya kifedha kidigitali kwa kufungua matawi zaidi ya 263 pamoja na mawakala zaidi ya 8,000 na benki hiyo kuongoza kifaida Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya benki hiyo, Ally Laay alisema benki hiyo imetoa gawio la asilimia 35 sawa na Sh bilioni 19.5 kwa serikali ili kuboresha huduma mbalimbali za maendeleo.Alitoa rai kwa watanzania kuwa na utamaduni wa kununua hisa ili waweze kuvuna gawio kila mwaka Alisema bado wananchi wengi hawaamini katika gawio la hisa au hununua hisa, bali wanawekeza zaidi katika miradi mingine ya maendeleo, hivyo ni vyema elimu zaidi ya itolewe shuleni na maeneo mbalimbali juu ya ununuzi wa hisa ili waweze kujikwamua kiuchumi hapo baadaye.
3
KOCHA msaidizi wa timu ya Yanga Noel Mwandila baada ya kupata pointi tatu dhidi ya Coastal Union mwishoni mwa wiki iliyopita, amsema rasmi sasa wamefungua mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa mwaka 2019/20.Yanga iliibuka na ushindi huo kwenye uwanja wa Uhuru Dar es Salaam baada ya kufanya vibaya katika mechi mbili za mwanzo ambapo ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Polisi Tanzania.Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha pointi nne ikiwa nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 20. Simba ndio inaongoza msimamo wa kuwa na pointi 12.Mwandila alisema walianza ligi hiyo kwa kusuasua kwa kupoteza mchezo mmoja na mwingine kutoka sare hivyo walipoingia kwenye mchezo uliopita aliwapa maelekezo wachezaji wake kuingia na jambo moja la kusaka pointi tatu muhimu.“Tumefanikiwa kupata pointi tatu muhimu ambazo tulikuwa tumedhamiria kuzipata na sasa tunatangaza tumeanza rasmi mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania,” alisema Mwandila anayeongoza benchi la ufundi kufuatia kocha mkuu wa timu hiyo Mwinyi Zahera kuendelea kutumikia adhabu aliyopewa na Bodi ya Ligi kwa kosa la kuvaa mavazi yasiyoruhusiwa uwanjani na kuwakejeli viongozi wa TFF.Katika hatua nyingine wachezaji wa kikosi hicho walizawadiwa kitita cha Sh. Million 10 kurudisha morali ya kuendelea kupambana na kila mchezo kuhakikisha wanapata pointi tatu muhimu.Fedha hizo zilitolewa na mdhamini wa timu hiyo GSM na kukabidhiwa na mwenyekiti wa timu hiyo Mshindo Msolla aliyedai kila timu hiyo watakapo kuwa wanavuna pointi tatu basi zitakuwa zinanunuliwa kwa kitita cha sh milioni 10.
4
JESHI la Polisi mkoani Njombe limesema mpaka sasa linawashikilia watu 27 wanaotuhumiwa kujihusisha na mauaji ya watoto mkoani humo.Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Renatha Mzinga, alipozungumza na Habarileo kwa njia ya simu.Kamanda Mzinga amesema, watu hao 27 wanashikiliwa kutokana na kuhusishwa na mauaji hayo.Aliongeza kuwa, katika uchunguzi wao, wamebaini viini vya mauaji hayo kuwa ni visasi, ugomvi wa mali kati ya ndugu na imani za kishirikina.Alisema operesheni ya jeshi hilo, bado inaendelea ili kubaini wahusika zaidi wa mauaji hayo na sababu zingine, zinazowafanya kuendesha mauaji hayo ya watoto.Kwa mujibu wa Mzinga, tatizo jingine walilolibaini ni kwa wazazi kutotoa taarifa mapema kwa Jeshi la Polisi, pale wanapobaini watoto wao hawaonekani.Alisema mtoto anaweza kupotea kwa siku tano, lakini mzazi hatoi taarifa yoyote na matokeo yake watoto hukutwa wameshauawa.Alisema miongoni mwa watuhumiwa wanaoshikiliwa ni yule aliyehusika na mauaji ya watoto watatu wa familia moja. Mwingine ni yule aliyehusika na mauaji yaliyotokea mwishoni mwa wiki.Kwa kuwa kesi zinazohusiana na mauaji zinahitaji kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli, Kamanda Mzinga alisema watuhumiwa hao, watafikishwa mahakamani, pale tu upelelezi utakapokamilika.Wiki iliyopita, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, alimwagiza Mkuu wa Jeshi Polisi nchini (IGP), Simon Sirro, kutuma timu maalumu ya upelelezi kutoka Makao Makuu ya jeshi hilo kwenda kuungana na timu ya wapelelezi ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe, kuchunguza matukio ya mauaji ya watoto mkoani humo.Masauni alikuwa mkoani humo kufuatilia mauaji hayo na kisha kumwagiza IGP Sirro kupeleka timu hiyo haraka ili kwa kushirikiana na timu ya wapelelezi wa Mkoa wa Njombe, wawakamate watu wote waliohusika na mauaji hayo ya watoto na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.Gazeti hili liliripoti wiki iliyopita kuzuka kwa taharuki katika mkutano wa naibu waziri huyo na wananchi wa wilaya ya Njombe, baada ya kusikika milipuko ya mabomu ya machozi, jirani na mkutano huo, hali iliyowafanya wananchi kukimbia hovyo na wengine kuelekea kwenye tukio.Baada ya wananchi hao kurudi kwenye Uwanja wa Turbo ili kuendelea na mkutano, walipinga kauli ya Polisi kuwa walikuwa wakipambana na wezi wa bodaboda.Walimweleza Masauni kuwa Polisi walikuwa wakiwatawanya wananchi, waliotaka kumpiga na kumuua mama mmoja aliyekamatwa akiwa na mtoto mdogo aliyekuwa akilia, kwa madai kuwa alitaka kumchinja.Kutokana na mkanganyiko huo wa taarifa, ndipo Masauni alipoamuagiza IGP kutuma timu maalumu ya uchunguzi, ambayo pamoja na mambo mengine, ijikite katika kuchunguza tukio hilo ili kujua kiini na uwiano wa nguvu iliyotumika na polisi, na uhalisia wa tukio lenyewe.
3
MANCHESTER, ENGLAND MICHUANO ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya inatarajia kuendelea leo kwa baadhi ya michezo kwa kuzitafuta timu ambazo zitaingia hatua ya 16 bora. Kuna klabu ambazo tayari zimetangulia katika hatua hiyo kama vile Real Madrid, Barcelona, PSG, Juventus, Man City, Bayern Munich na Zenit. Kivumbi ni leo kwa Klabu ya Manchester United ambayo itashuka dimbani dhidi ya Wolfsburg katika kundi B, huku kila timu ikihitaji ushindi ili kujihakikishia inaingia 16 bora. Wolfsburg wanaongoza kundi hilo wakiwa na alama 9 wakati United ikiwa na alama 8 ikifuatiwa na PSV yenye alama 7. Kama United itapoteza mchezo itawapa nafasi PSV endapo itashinda katika mchezo wake dhidi ya CSKA Moscow, ambapo wakishinda PSV itakuwa na alama 9, hili ni kundi gumu kwa timu hizo kutokana na tofauti ya alama. Katika kundi C, kazi itakuwa nyepesi kwa timu ya Benfica na Atletico Madrid, hapa timu zote zina alama 10 katika kundi lao. Timu hizo zinafuzu hatua ya 16 kwa kuwa wapinzani wao kwenye kundi hilo Galatasaray wana alama 4 wakati huo Astana wakiwa na alama 3, ambapo itakuwa ngumu kwao kufuzu katika michezo yao ya leo. Michezo mingine ambayo itapigwa leo ni pamoja na Man City ikipambana na Monchengladbach, Real Madrid dhidi ya Malmo, Sevila dhidi ya Juventus, huku PSG ikicheza dhidi ya Shakhtar.
4
Na RASI INNO NGANYANGWA KAMA kuna wengi wanaofahamu kuhusu ‘Back’ yake katika kuzimikia muziki nina hakika ni wachache sana kutokana na hulka yake ya ‘non nosense’ tangu kitambo akiwa katika nafasi mbalimbali za uwaziri. Lakini hiyo sio ishu ninayotaka tuisanukie hapa leo kwani politiki siyo mahala pake katika safu hii, ila akiwa kama mkuu wa taifa kuna hisia zilimgubika akaweka wazi kwamba hazimikii masuala ya masholi kujiachia kihasara kwenye vichupa. Kwa hali ilivyo ni kwamba huwezi kucheki kichupa na mtu unayempa respect kubwa manake jinsi video vixens wanavyojiachia inaleta hisia nyingine zisizotakiwa hadharani ambazo mahala pake ni faraghani. Wakati akipiga nondo hiyo alikuwa akinena na wanachama wa CCM kwenye mkusanyiko wao kule Dodoma, tangu hapo alichokianzisha kikashika kasi hata walio chini yake wakawa wanapigia upatu. Prezidaa alinena kwamba hata yeye anazimikia sana mangoma ila vichupa vinamboa kutokana na mambo hadharani yanayofanyika ambayo hayafai! Ikanipa aidia kwamba nikague vichupa kadhaa vinavyoruka hewani kwenye runinga ambavyo katika ‘Back’ hiyo ilikuwa poa tu katika awamu zilizopita, kwamba ilikuwa kawaida tu kuwa kihivyo lakini tangu mkubwa aseme yake kuhusu hiyo ishu kuna vichupa kadhaa katika ‘Front’ iliyofuata vimejikataa vyenyewe. Hata kama vikilazimishwa kuwekwa kwenye kioo cha runinga ama vitakatizwa chata la utata linapokaribia au vitafanyiwa mixing ya kiaina ili kuziba au kichupa kingine kinapandishwa juu yake na kukiziba kichupa fyongo. Hiyo maana yake ni kwamba kuna wasanii kadhaa itabidi watengeneze video mpya kwani zilizowapaisha kama zina mambo ya misanuko aliyokemea Prezidaa mida ya sasa katika ‘Front’ hii sio mwake kabisa! Hapo mambo ya bajeti yanahusika na kama nd’o ilikuwa ya unga unga mwana basi lazima kwenye ‘Front’ mpya kuna wasanii watabonyea kwa muda. Hii ishu imenirudisha ‘Back’ nyakati flani ilipoaminika kwamba ‘obscenity sales’ kwamba misanuko wazi inauza! Lakini kama kila kitu ni kukopi na ‘ku-paste’ basi kiaina tunatokota, maana sio kila kitu cha kukopi, kwani hata huko mbele kuna maneno yanayotumika kwenye mistari tangu kitambo hadi sasa utayakuta kwenye mauzo ya kitaani. Sio kwenye kucheki kwa ujumla kama ambavyo neno ‘F’ lisivyotumika kila mahala kama inavyodhaniwa ndiyo maana kule wana ‘system’ ya kudhibiti kisichotakiwa kuchekiwa na madogo ili wasipagawe tangu mapema. Prezidaa sio myuzishen ila anazimikia tu mangoma lakini amegusa na katika ‘Front’ hii lazima jambo lifanyike manake kuna wasanii ni kama wanasukuma muziki wao kwa kujianika, kana kwamba hiyo ndiyo biashara halisi kumbe ni kinogesho tu uhalisia uko kwenye mikong’osio yenyewe. Kwenye kadanse ndiko ‘live’ misanuko hatari ya madensa wa kike hujitokeza lakini kwenye kizazi kipya huanzia kwenye vichupa, hata kama uko homu na madogo inakulazimu kubadili chaneli kukwepa msala wasikuulize kisha ukashindwa kuwajibu. Madogo wa leo sio kama wa zamani zile kwani kama wasanii wanajiita kioo cha jamii basi kimewapasukia usoni!
1
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema, Mbunge wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto anampa taabu sana na ameomba ushauri amfanye nini.Ndugai amesema jijini Dar es Salaam kuwa, Zitto anampa taabu kwa sababu chama cha ACT Wazalendo kina Mbunge mmoja tu kwenye Bunge la Tanzania hivyo akimfukuza chama hicho kitakosa uwakilishi bungeni.“Niseme ukweli huyu amekuwa akinipa taabu sana, nisema tu ukweli wa moyoni kwa sababu ni Mbunge wa kipindi karibu cha tano anapaswa kuwa anafahamu mambo mengi”amesema.“Sasa huyu yaani ni mmoja tu kwenye chama chake, ukifukuza hakuna tena uwakilishi na mtaniuliza maswali waandishi maana yake ninyi hamchoki, sasa huyu umemfukuza mzee sasa, kwa hiyo wakati mwingine nahitaji hata ushauri wenu, hivi mtu kama huyu unamfanyaje…“he he he, hee chama ambacho kina Mbunge mmoja tu, sasaa heeh, maana sio minority tena, yaani ni, si jui nini, katika wabunge 393 karibu na mia nne yaani mmoja tu, ndiyo maana mnamuona anahangaika mahakamani peke yake tu”amesema Spika Ndugai.Amesema Zitto anahangaika na mambo yake peke yake kutafuta umaarufu, bado hajafikiria kumuita, watamvumilia ila ipo siku watachukua hatua.“Yupo huku Dar es Salaam wenzake wapo Dodoma, anadanganyadanganya watu huku, kuzunguka zunguka kwenye makorido, kaenda na kesi ya ajabu ajabu ile, sijui ya vyama vya siasa imeenda wapi. Na ule muswada upo kule niwaambieni unaendelea kama kawaida, sasa hivi kwenye ngazi ya kamati, likianza Bunge muswada unaingia”amesema Ndugai.
3
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza awamu ya kwanza ya wanufaika wa mikopo yenye waombaji 25,532, waliopangiwa mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 88.36 kwa mwaka wa masomo 2018/2019.Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul- Razaq Badru alisema kati ya wanafunzi hao, wanaume ni 16,085 na wanawake ni 9,447.Badru alisema katika awamu hiyo ya kwanza, HESLB imetoa mikopo yenye thamani ya Sh milioni 850.35 kwa wanafunzi 69 wanaoendelea na masomo nje ya nchi chini ya makubaliano maalumu na nchi rafiki saba zikiwemo Msumbiji, Algeria, Cuba, Urusi, Serbia, Ukraine na Ujerumani.Alisema bajeti ya fedha za mikopo ya elimu ya juu zilizotengwa kwa mwaka wa masomo 2018/2019 ni Sh bilioni 427.5. Alisema tayari serikali imetoa Sh bilioni 137.06 zinazohitajika wakati vyuo vinafunguliwa mwishoni mwa mwezi huu na mapema mwezi ujao ili kuwakopesha wanafunzi wapya na wanaoendelea na masomo wapatao 123,285.“Fedha nyingine tunazipokea baadaye katika robo ya pili ya mwaka wa fedha kwa ajili ya malipo ya wanafunzi watakaopangiwa mikopo... hivyo kwa sasa tuna fedha tunazohitaji kwa waombaji wote wenye sifa,” alieleza.Alisema katika wanafunzi hao 123,285, wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza ni 40,285 na tayari fedha yote imepatikana ili kuondoa uwezekano wa wanafunzi kupoteza muda katika usumbufu wa kufuatilia mikopo.Alisema orodha ya walioomba mikopo ni 41,000 na waliopata kwa awamu hii ni 25,532. Kuhusu kutangazwa awamu ya pili, alisema wataendelea kutoa orodha za wanaopangiwa mikopo kadri watakavyokamilisha uchambuzi wa wanafunzi walioomba mikopo na ambao pia wamepata na kuthibitisha udahili wao katika chuo kimoja ili kuhakikisha fedha za mikopo zinawafikia wahitaji katika vyuo walivyothibitisha.“Baada ya kutangaza orodha waliyodahiliwa, baadaye tutafungua dirisha la kukata rufaa kwa wale ambao hawakuridhika, tutafungua Novemba Mosi hadi 15, zamani rufaa ilikuwa ni miezi mitatu ila sasa tunafanya kwa muda mfupi ili nao waweze kupata fursa ya kusoma kwa wakati,” alisema mtendaji huyo wa HESLB.Alisema majina yote ya waombaji waliopangiwa mikopo katika awamu hiyo ya kwanza, yataweka katika mtandao wa HESLB wa uombaji wa mkopo na tovuti ya bodi na pia orodha ya majina hayo itatumwa vyuoni kwa ajili ya kurahisisha taratibu za usajili wa wanafunzi hao.“Lengo la bodi ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wenye sifa ya kupata mikopo katika mwaka wa masomo 2018/2019 wanapangiwa mikopo kabla ya vyuo kufunguliwa mwishoni mwa Oktoba, mwaka huu,” alisema.Mwaka wa masomo wa 2018/19 unaanza Oktoba 29, mwaka huu. Pia aliwasihi waombaji wa mikopo kuwa watulivu wakati mchakato wa upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye sifa kwa awamu inayofuata ukiendelea.Akizungumzia upangaji mikopo kwa wanafunzi wa mwaka wa pili na kuendelea, Mkurugenzi wa Uchambuzi na Upangaji Mikopo wa HESLB, Dk Veronica Nyahende alisema wanafunzi wenye mikopo na wanaoendelea na masomo, wataendelea kupata mikopo ikiwa wamefaulu mitihani na matokeo kuwasilishwa bodi na vyuo husika.“Tunatoa mikopo ili mwanafunzi asome, kwa hiyo tutaendelea kuwapa mikopo wanafunzi wenye mikopo na wanaoendelea na masomo ikiwa tumepokea uthibitisho kuwa ana sifa za kuendelea na masomo katika mwaka unaoanza hivi punde,” alisema Dk Nyahende.Alisema wanafunzi 83,000 wanaoendelea wanapatiwa mikopo baada ya kuthibitishwa kama wamefaulu na wanaendelea na masomo, na matokeo hayo huambatana na barua na vielelezo kutoka kwa mkuu wa chuo. Hata hivyo, alisema hadi sasa vyuo 10 ambavyo hakutaka kuvitaja alisema havijapeleka matokeo, hivyo wanafunzi wa vyuo hivyo wanaweza kuchelewa kupata mkopo.
3
UJIO wa Kocha wa Simba, Sven Vandenbroeck, umezidisha matumaini ya mafanikio kutokana na mbinu na mifumo anayowafundisha wachezaji wake ikiwa ni siku nne tangu alipoanza kuifundisha timu hiyo.Vandenbroeck amezungumza na gazeti hili na kukiri Simba ina wachezaji wenyeji vipaji isipokuwa anachokifanya ni kuwajenga katika utimamu wa mwili, kimbinu na mifumo watakayotumia ili kuhakikishia wanapata matokeo ya ushindi kwenye mechi.“Nina siku chache tangu nianze kazi lakini nimefurahi kuona Simba ina wachezaji wenye vipaji ingawa wengine wapo timu za taifa naamini kazi yangu haitokuwa ngumu kwa sababu nafanya kazi na watu wanaojua nini nataka kwa sasa tutafanya mazoezi magumu ili kupima utimamu,” alisema Vandenbroeck.Baadhi ya wachezaji wa Simba, licha ya kuhenyeshwa kwa saa tatu, wamemvulia kofia kocha huyo pamoja na msaidizi wake Seleman Matola na kueleza endapo mazoezi hayo yataendelea siku zote kuna uwezekano baadhi ya timu zikapata aibu ya mwaka kwa kuzifunga idadi kubwa ya mabao.Wakati Simba, wakitambia ujio wa kocha wao, watani zao Yanga nao mambo yamezidi kunoga baada ya kocha wa muda Charles Mkwasa, kuridhishwa na muunganiko wa kiuchezaji unaonyeshwa na wachezaji wake na kuwataka mashabiki kukaa mkao wa kula.Mkwasa alisema kadri siku zinavyokwenda Yanga imezidi kubadilika na anaamini mambo yatakuwa zaidi ya hapo baada ya kuongeza baadhi ya wachezaji kwenye dirisha dogo ambalo limefuguliwa jana.“Mashabiki wa Yanga, waondoe hofu kwani wana timu nzuri, mwanzo ulikuwa mgumu kwa sababu kuna wachezaji tuliwakosa kwenye timu lakini baada ya dirisha la usajili watakuwepo na muunganiko wa timu ni mzuri,” alisema Mkwasa.
4
ASASI za kiraia ni taasisi huru zilizoundwa kwa mujibu wa sheria mbali mbali nchini. Zinatekeleza majukumu yake katika kuhakikisha ustawi wa taifa. Serikali inatambua kuwa asasi za kiraia ni muhimili muhimu kwenye kuhimiza maendeleo ya jamii na kubuni miradi mbali mbali kwa ajili ya kuwezesha jamii hasa vijana na wanawake kwa maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.Asasi za kiraia iliyohai huwakilisha kwa kusaidia mfumo wa maridhiano na uazishwaji na usimamizi wa sera za maendeleo endelevu na ukuaji shirikishi wa uchumi wa nchi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.Umoja wa Ulaya umekuwa ukisaidia asasi za kiraia zikiwamo za Tanzania katika kipindi kati ya mwaka 2014 na mwaka 2020. Umoja huo na nchi wanachama zinafadhili Euro bilioni 1.97 kwa shughuli zinazoanzishwa na asasi za kiraia duniani.Hii inatia nguvu na kuonesha wazi kwamba asasi za kiraia ni muhimili na sauti ya jamii; chachu ya mabadiliko ya kisera kwa kuibua changamoto. Visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla asasi za kiraia zina wajibu mkubwa ambao unaweza kuonekana katika kuleta mabadiliko na kutatua changamoto ambazo zinaikabili jamii kupitia asasi hizo.Msajili wa Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) Zazibar, Dhamir Kombo Hamadi anasema serikali imetoa fursa kwa wananchi kujiunga na kusajili mashirika mbali mbali zikiwamo asasi za kiraia zenye dhamira moja yakinifu katika kumulika jamii kupitia changamoto ziazozikabili na kuzitafutia ufumbuzi.Dhamir anasema ni vyema kuibua hamasa ikiwamo uwajibikaji wa taasisi au jumuiya na mikakati yenye malengo ambayo yataleta mabadiliko endelevu katika kusaidia serikali pale ambapo haikupitisha mkono wake kwa faida ya taifa .Mbali na kuibua mwamko, Dhamir anasema mara nyingi jumuiya ambazo zinafuata taratibu za kisheria ndiyo zinazopiga hatua katika kutatua changamoto na kufuata taratibu endelevu na msimamo thabiti ya kutoa ushirikiano wa pamoja na afisi ya mraji katika kuleta mabadiliko juu ya kutoa maendeleo ya taarifa zao kwa kila kipindi fulani katika mwaka.Anasema sehemu yoyote duniani, iwe taasisi, jumuiya, au mashirika ya umma, ni lazima kuwe na utaratibu maalumu wa kufuata sheria ili kwenda sambamba na malengo waliojiwekea na kuweza kufika kwa wepesi pale wanapokwama jambo ambalo ni la kuzingatiwa.Mrajisi anasema ofisi yake sasa kupitia utaratibu mpya wa usajili wa N G Os, inatilia mkazo baadhi ya jumuiya ambazo hazijajisajili zikafanye hivyo kuepuka kufutwa mwishoni mwa mwaka huu hali ambayo itakayokatisha tamaa juhudi za jumuiya husika. “Kutii sheria ni suala la msingi kwa asasi za kiraia ili kuepuka vikwazo na kusababisha kutoweza kufutwa kabisa”anasisitiza Dhamir.Anasema jumuiya zilizosajiliwa na ofisi ya mrajisi Zanzibar ni 2,864 kulingana na sheria namba 6 ya 1995 ya usajili wa N G O. Katibu Mkuu wa Jumuia ya wasioona Zanzibar ( ZANAB), Adil Mohammed Ali anasema ni vyema jumuiya zikajitahidi katika kufanya kazi zake kwa weledi zaidi. Anaonya jumuia za mifukoni ambazo hazina ofisi maalumu kwa maana ya NGO za mfukoni. Anazitaka jumuiya zote kujijengea uaminifu zisitiliwe mashaka na kuzorotesha utendaji wao. “Ni moja ya maendeleo kuwa na usajili kwa njia ya mtandao na kunaweza kuleta matokeo chanya” anasema Ali.Anasema kupitia haya ipo haja ya kila jumuiya kufahamu wajibu wake kwa kuwasilisha taarifa zao kwa mrajisi kutatua changamoto zao kwa urahisi pindi zinapojitokeza na kuwa miongoni mwa jumuiya zinazojitambua ziwe mfano kwa jumuiya nyengine .Hatua nyingine ni uandaaji wa maendeleo ikiwamo utoaji wa taaluma zaidi na usimamizi wa sheria kufikia lengo lililokusudiwa na siyo ubinafsi na ubabaishaji ili taifa linufaike kwa uwepo wa asasi hizo.Ofisi ya mrajisi Zanzibar imeweza kuendeleza vipindi maalumu kupitia vyombo vya habari vinavyotoa elimu hasa elimu ya usajili mpya iIi kwenda sambamba na zama hizi za kidijiti.
3
WACHIMBAJI, wafanyabiashara na wadau wa sekta ya madini nchini, wamemkabidhi Rais John Magufuli mapendekezo 22, yatakayosaidia kudhibiti utoroshaji wa madini na kuongeza mapato ya serikali.Mapendekezo hayo yaliyokabidhiwa juzi jijini Dar es Salaam kwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya rais katika Mkutano Mkuu wa Kisekta wa Madini, ni pamoja na kutaka Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ya asilimia 18 ifutwe. Mapendekezo mengine ni tozo ya zuio kupunguzwa kutoka asilimia tano hadi kufikia asilimia tatu, tozo ya ushuru wa halmashauri iongezwe kutoka asilimia 0.3 hadi kufikia asilimia moja na mrabaha kupunguzwa kutoka asilimia sita hadi kufikia asilimia tatu.Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini (FEMATA), John Bina, alitaja mapendekezo mengine ni madini ghafi ya vito, yaruhusiwe kusafirishwa nje ya nchi ili kuondoa ushawishi na utoroshaji wa madini hayo kwenda nje ya nchi. Pia, kuanzishwa kwa benki ya madini, maofisa wa madini kuwepo katika maeneo ya uzalishaji wa madini ili kuimarisha usimamizi na ukusanyaji wa mapato ya serikali.Katika hali ya kuifanya sekta ya madini kuzaliwa upya, wachimbaji hao pia walipendekeza serikali itoe ruzuku ya vifaa kwa wachimbaji wadogo wa madini, madini yanayotoka nje ya nchi yaingizwe nchini bila kutozwa tozo yoyote, lakini yanapotoka kwenda nje ya nchi yatozwe kodi zote zinazotakiwa, ada ya mwaka ya malipo ya eneo la wachimbaji kwa hekta ipunguzwe kutoka Sh 80,000 hadi kufikia Sh 50,000.Kwa mujibu wa wadau hao wa madini, gharama ya ada ya leseni ya uchenjuaji ipunguzwe kutoka dola za Marekani 1,000 hadi kufikia dola 500, uhai wa leseni za uchimbaji mdogo uongezwe kutoka miaka saba hadi kufikia miaka 15, ufanyike ulinganifu wa tozo za kodi kwa nchi za Maziwa Makuu na zilipwe mara moja na kwa taasisi moja pamoja na bei ya dhahabu iwe chini ya bei ya soko la dunia kwa soko la ndani. Kwa kuwa dhahabu inaweza kusafirishwa kutoka sehemu moja hadi nyingine ndani ya nchi kwa lengo la kutafuta masoko, wadau hao wa madini walipendekeza waruhusiwe kufanya hivyo kwa vibali maalumu.Pia vibali vya mazingira vitolewe wakati leseni za uchimbaji zinapotolewa na wamiliki wa leseni watakapobainika kutorosha madini, wafutiwe leseni zao na washitakiwe kama wahujumu uchumi. Alisema baada ya maazimio waliyoyafikia kwenye mkutano huo, mtu yeyote miongoni mwao atakayebainika kutorosha madini, atafukuzwa kwenye umoja wao. Pia, aliiomba serikali kuyafanyia kazi mapendekezo yao kwa haraka ili utekelezaji uanze. Waziri wa Madini, Doto Biteko, aliwataka wadau hao wa madini kuhakikisha wanasimamiana ili kudhihirisha nia njema waliyonayo kwa serikali.
3
Diamond ambaye nyota yake imekuwa iking’ara kila kukicha, alitwaa tuzo tatu ambazo ni Tuzo ya Msanii Bora wa Afrika, Tuzo ya Wimbo Bora Unaochezwa kupitia kibao chake cha Nana na nyingine ikiwa Tuzo ya Msanii Bora wa Afrika Mashariki.Alipowasili katika Uwanja huo jana, msanii huyo alikutana na maelfu ya mashabiki uwanjani hapo ambao walikuwa wakimshangilia kwa kupiga kelele. Alipotoka nje ya uwanja mashabiki wake hao walimbeba na kuanza kukimbia naye hadi nje kidogo ya eneo la kupokelea wageni ambapo alizungumza na waandishi wa habari.Huku akiwa anazungumza na waandishi wa habari mashabiki wake hao waliendelea kupiga kelele za kumshangilia hali iliyosababisha kukatisha mara kwa mara mahojiano baada ya nyota huyo na wanahabari.Baada ya mahojiano hayo, mashabiki hao walimbeba na kuanza kukimbia naye ambapo walitoka naye hadi nje kabisa ya geti kuu la kuingilia na walimpeleka hadi nje ya Uwanja na kuanza msafara wa kuondoka kuelekea ufukwe ya Escape One, Mikocheni.Msanii huyo alipitia njia ya Tazara kisha kuelekea njia ya Buguruni na kupitia njia ya Kigogo kuelekea Magomeni kwenda Mikocheni kwenye fukwe ya Escape One.Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Huduma ya Tigo Music, Hamza Balla ambapo huduma hiyo imekuwa ikiunga mkono jitihada za Diamond katika kujitangaza kimataifa alisema ushindi huo wa Diamond umefungua sura mpya kwa huduma hiyo.Alisema huduma hiyo imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu zaidi na Diamond na mashabiki wake katika kumtangaza na kumwombea kura katika mashindano mbalimbali anayoshiriki.
4
Katika fainali ya wasichana, Dar es Salaam walitawazwa mabingwa baada ya kuwatandika bila huruma Mashariki kwa mabao 7-1 kwenye mchezo uliokuwa na msisimko mkubwa kwa Dar es Salaam kuonesha uwezo mkubwa.Dar es Salaam ilitinga fainali baada ya kuisukumiza nje Kanda ya Ziwa mabao 4-1 huku Mashariki ikitinga katika fainali baada ya kuifunga Kaskazini kwa mabao 3-1.Kwa upande wa fainali ya wavulana, Nyanda za Juu Kusini walitawazwa mabingwa baada ya kuifunga Dar es Salaam bao 1-0, wakijifunga baada ya mabeki wa Dar es Salaam kujichanganya katika harakati za kuokoa hatari langoni mwao.Nyanda za Juu Kusini walitinga fainali baada ya kuifunga Kanda ya Ziwa kwa mabao 3-0 huku Dar es Salaam wakitinga hatua hiyo baada ya kuifunga Zanzibar ambao ndio walikuwa mabingwa watetezi kwa mabao 4-3.Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) chini ya Mwenyekiti wake Almas Kasongo, kimeelezwa kufurahishwa kwake na mafanikio yaliyooneshwa na vikosi hivyo vilivyo katika himaya yake.Imeziomba klabu za ligi mbalimbali kujitokeza kuangalia mashindano ya vijana ili kupata wachezaji wao wa baadaye.
4
MICHUANO ya mabenki kwa mpira wa kikapu (Bankers Basketball League – BBL 2018), imezidi kushika kasi, ambako mwishoni mwa wiki kikosi cha NMB kiliichapa CRDB kwa pointi 52-42.NMB chini ya Kocha Mkuu Evarist Mapunda, ilitawala kwa kiasi kikubwa pambano hilo lililofanyika kwenye Viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, ambako walimaliza nusu ya kwanza ya mtifuano huo wakiwa mbele kwa 26-15.Katika nusu ya pili, kujiamini kulikopitiliza kuliwafanya nyota wa NMB kupunguza kasi, ambako walijikuta wakimaliza nusu hiyo hiyo kwa kipigo cha 27-26, ingawa havikutosha kuwapa CRDB ushindi wa jumla, hivyo NMB kushinda 52-42.Akizungumza baada ya mchezo, Kocha wa NMB, Mapunda aliwapongeza nyota wake kwa upambanaji uliofanikisha kuibuka na ushindi huo na kwamba wamejipanga kuhakikisha wanautwaa ubingwa wa michuano hiyo inayofanyika kila mwaka.“Tumetimiza lengo la kuibuka na ushindi katika mechi dhidi ya CRDB, nawaponeza nyota wangu kwa upambanaji, na sasa tunaelekea kwenye mazoezi kujiandaa na mechi zijazo kulingana na ratiba, ili kufanikisha lengo kuu la kutwaa ubingwa,” alisema Mapunda.Kabla ya NMB kuichachafya CRDB, pambano la awali juzi lilizikutanisha DTB na TADB, ambako kikosi cha DTB kiliibuka na ushindi wa pointi 73-40, ambako washindi waliongoza kwa 40-16 katika nusu ya kwanza, kisha 33-24 katika nusu ya pili.Mbali na mpira wa kikapu, pia NMB iliwafunga timu ya mpira wa miguu ya CRDB kwa magoli 3-0 katika mchezo uliopigwa mapema na kufuatiwa na mpira wa mikono.
4
  NA CHRISTOPHER MSEKENA VIDEO zimekuwa chanzo kipya cha mapato kwa wasanii wa Bongo Fleva na sasa hawategemei kuuza audio pekee kama ilivyokuwa hapo awali. Zamani msanii alitoa video ili kukamilisha utaratibu, lakini sasa imekuwa tofauti kwani msanii anapotoa wimbo analenga kuingiza fedha kwenye audio na video kwa pamoja. Mtandao wa Youtube ni soko kuu la wasanii kuuza video zao za muziki, kupitia matangazo yanayoonekana kabla ya video kuanza, asilimia flani zinaingia kwenye kibubu cha msanii, kwa kila watazamaji elfu moja wa video basi msanii huyu anatengeneza nusu dola hadi dola moja ya Marekani. Kwa hiyo kadri video ya muziki inapotazamwa na watu wengi ndiyo hivyo anavyozidi kujipatia fedha. Ndiyo maana siku hizi wasanii wengi wamekuwa wakiwekeza zaidi kwenye video sababu ni soko jipya la kazi za muziki na malipo hayo yapo tu kwa wasanii waliosajiliwa kwani vigezo na masharti huzingatiwa. Sasa Juma3tata leo tunakusogezea video tano za muziki ambazo zimetoka wiki mbili zilizopita na kwa muda mfupi zimetazamwa mara nyingi zaidi na kufikisha watazamaji zaidi laki 2 hivyo kumuingizia msanii husika mkwanja kwa muda mfupi   Harmonize- Sina Ni video iliyoachiwa Julai 27 mwaka huu, ndani ya siku saba tayari ilikuwa imefikisha watazamaji milioni 1, inawezekana mafanikio ya wimbo huu yametokana na uwepo wa Mr Nice katika video, akiingiza maisha ya kijana aliyekuwa na fedha nyingi na baada ya matanuzi na starehe mbalimbali akajikuta amekuwa masikini. Video ya Sina imefanyika hapa hapa Bongo na kuongozwa na Khalfan Khalmadro. Aslay- Baby Huu ni wimbo wake wa nne aliouachia mfululizo ndani ya miezi mitatu. Baby ni ngoma nyingine kali ambayo aliiachia Julai 19 mwaka huu na mpaka sasa video yake imetazamwa na watu laki 6. Video ya Baby imetengenezwa hapa hapa Bongo na kuongozwa na Einxer, mwongozaji ambaye anakuja kwa kasi sana kwenye utengenezaji wa video za Bongo Fleva baada ya kufanya video nyingi za muziki wa Injili. Rich Mavoko ft Fid Q- Sheri Baada ya wimbo wao na Harmonize, Show Me kupata mafanikio makubwa, Mavoko ameachia ngoma aliyomshirikisha Fid Q inayoitwa Sheri na video yake imetoka Julai 24 mwaka huu. Mpaka sasa imetazamwa na watu laki 598,500, ikiwa ni kazi nzuri ya mwangozaji mtanzania, Joowzey. Joh Makini ft Davido- Kata Leta Ni kolabo ya tatu ya kimataifa ya rapa Joh Makini, amewahi kufanya wimbo na AKA kutoka Afrika Kusini na Chidima kutoka Nigeria na sasa kwenye Kata Leta amemshirikisha msanii Davido. Video umefanyika Afrika Kusini na ameitoa Julai 23 mwaka huu ambapo ndani ya siku chache sasa imetazamwa na watu zaidi ya laki 4. Country Boy ft Mwana Fa- Turn Up Ni wimbo ambao umejipatia umaarufu katika sehemu mbalimbali za starehe, Turn Up ngoma ambayo imefanikiwa zaidi kutoka kwa msanii, Country Boy akiwa amemshirikisa Mwana Fa. Video ya Turn Up imetoka Julai 19 mwaka huu na ndani ya siku chache imetazamwa na watu na zaidi ya laki 2. Imefanyika Afrika Kusini na kuongozwa na mtanzania, Hanscana.  
1
MCHUNGUZI Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Frank Mkilanya ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Klabu ya Simba, Zacharia Hanspoppe, alimueleza kuwa alitumia Dola za Marekani 32,316.64 kulipia malipo ya awali wakati wa ununuzi wa nyasi bandia za klabu hiyo.Mkilanya amedai katika Mahakama ya Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati akitoa ushahidi wake katika kesi inayowakabili vigogo wa klabu hiyo.Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Leonald Swai, shahidi huyo alidai katika ununuzi wa nyasi hizo, Hanspoppe ndiye alianzisha mchakato wa ununuzi wa nyasi hizo pamoja na kufanya mawasiliano kati ya mnunuzi na muuzaji.Amedai wakati akiandika maelezo ya mshitakiwa huyo wa tatu, alimueleza kuwa walinunua nyasi hizo kutoka kwa wakala anayetambulika kwa jina la Hamis kutoka China aliyenunua nyasi hizo kutoka kampuni ya Ninah Trading Company.“Kesi hii ilianza kufunguliwa kabla ya kuandika maelezo ya mshitakiwa kwakuwa alikuwa hajapatikana lakini baada ya kupatikana ndio maelezo yake yakachukuliwa na hayo ndio nilichukua,” alidai Mkilanya.Alidai, hundi ya manunuzi ya nyasi inaonesha zilinunuliwa kwa Dola za Marekani 109,499 ambapo Hanspoppe baada ya kupata hundi hiyo alifanya malipo ya awali ya Dola za Marekani 32,316.64 kwa fedha zake binafsi.Mkilanya alidai, mshitakiwa huyo alimueleza kuwa hundi hiyo baadaye alimkabidhi aliyekuwa rais wa klabu hiyo Evans Aveva na wakala (Hamisi) alipokuja nchini na kumpa fedha taslimu Dola za Marekani 15,000.Alidai kuwa, Hanspoppe alimueleza kuwa wakala huyo ameshafariki.Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi kesho kwa ajili ya kusikilizwa. Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni aliyekuwa makamu wa rais wa klabu hiyo Godfrey Nyange ‘Kaburu’.Washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka 10 ikiwemo kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za kughushi, kutoa maelezo ya uongo na utakatishaji wa fedha.Katika shitaka la kughushi linawakabili washitakiwa wote, inadaiwa katika tarehe hizo hizo kwa pamoja walighushi hati ya malipo ya kibiashara ya Mei 28, 2016 wakionyesha kwamba nyasi bandia zilizonunuliwa na Simba zenye thamani ya Dola za Marekani 40,577 sawa na zaidi ya Sh milioni 90 huku wakijua kwamba sio kweli.Pia katika mashitaka mengine inadaiwa Aveva, Nyange na Hans Poppe kati ya Machi 10 na Septemba 30, 2016 waliwasilisha nyaraka za uongo kuonyesha Simba imenunua nyasi bandia zenye thamani ya Dola za Marekani 40,577.
4
MSIMU wa 2019/2020 unaweza kusema ni furaha kwa wekundu wa Msimbazi, Simba kwa sababu wametimiza baadhi ya mambo yao huku Yanga ikiendelea kutaabika kwa kila kitu.Ukiachilia mbali kuongoza katika msimamo wa ligi, Simba imemaliza ujenzi wa awamu ya kwanza ya uwanja wao wa mazoezi uliopo Bunju unaofahamika kwa jina la Mo Simba Arena.Hilo ni jambo zuri na la kupongezwa baada ya kukaa miaka 83 bila kuwa na uwanja wake. Simba ya sasa si ile ya zamani, inajivunia uwekezaji wake chini ya Mohamed Dewji ambapo kwa sasa huwezi kusikia wachezaji wanalia njaa au ucheleweshaji wa mishahara kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.Pia, timu hiyo wanajaribu kujiendesha kisasa baada ya kubadilisha mfumo na kuingia kwenye kampuni. Hilo linajionesha wazi kutokana na namna wanavyopangilia mambo yao kuanzia kwenye kuajiri.Kwa sasa huwezi kulinganisha Simba na Yanga zimetofautiana kuanzia ubora, uwekezaji na mfumo. Simba ya sasa ina uwezo wa kusajili mchezaji yeyote wanayemtaka, changamoto iliyopo kwao ni namna wanavyosajili na kushindwa kupata wachezaji wanaostahili. Kingine uswahili mwingi kila mtu ana mchezaji wake wa kumsajili kwa ajili ya kupata ile asilimia 10 na hayo yanaweza kuwa hatari kwao.Sababu kubwa iliyonifanya nione kuna uswahili ni namna Kocha aliyetimuliwa Patrick Aussems aliwahi kusema kuwa kuna wachezaji aliwapendekeza kwa ajili ya kusajiliwa kabla ya kuanza kwa msimu huu lakini alivyorudi kutoka likizo alikuta mambo tofauti.Kati ya wachezaji sita au saba aliowahitaji alimkuta mmoja tu. Sasa inaonesha ni kwa namna gani mambo hayakuwa sawa. Matokeo yake ya sasa timu yao ikashindwa kufanya kile kitu ambacho walikitarajia kisha mzigo wa lawama wakamwachia kocha wao.Inawezekana kabisa kocha huyo alikuwa na makosa mengine kama ya nidhamu lakini kwa upande wa kiwango cha timu hakika wanaweza kulaumiana wote. Bado licha ya wekundu hao kuonekana hawachezi katika kiwango kinachohitajika, unaweza kusema ni miongoni mwa timu zilizoonesha jitihada katika mechi zao kadhaa zilizopita za ligi.Ukilinganisha na Yanga, kiwango ni tofauti. Simba ina wachezaji wengi wazuri na kikosi kipana tofauti na watani zao kuna baadhi ya wazuri lakini kuna muda wakifanya mabadiliko mambo yanazidi kuwa magumu badala ya kuwa mazuri.Utofauti wa Yanga kwa Simba ni kwamba, Yanga bado wanaendelea kulia njaa, kwa sababu wanakabiliwa na ukata. Si kwamba umeanza sasa hata kidogo bali tangu kuondoka kwa aliyekuwa Mwenyekiti wao wa zamani, Yusuf Manji. Yanga ina madeni kibao na kuna wakati wachezaji wanaliamsha wakiwa hawajalipwa mishahara. Ushahidi ni taarifa za hivi karibuni kuwa baadhi ya wachezaji kama Sadney Urikhob, Lamine Moro na Juma Balinya kuandika barua na kuomba kuvunja mkataba kwa sababu hawakulipwa mishahara ya miezi miwili.Mwenyekiti wa Yanga, Dk Mshindo Msolla anathibitisha ni kweli wanaelemewa na mzigo wa madeni na kutaja zaidi ya Sh bilioni mbili huku akisema madeni mengine aliyakuta. Hayo yote yanadhihirisha ni namna gani timu hizi mbili kwa sasa zinazungumza habari tofauti. Mwingine anacheka na mwingine analia hapo ndipo utofauti ulipo. Tabu ile ile Simba ilikuwa inataabika kupata matokeo mazuri katika baadhi ya mechi sawa na Yanga, licha ya wote kutamba kuwa walisajili wachezaji wazuri. Kingine fukuza ya makocha.Yanga ilianza kumtimua Kocha aliyekuwepo Mwinyi Zahera kisha Simba wakafuata na kuachana na Patrick Aussems. Isipokuwa sababu za kuwatimua makocha zinatofautiana kiasi lakini mengi ni yale yale tu na zaidi wakigusia kiwango cha uwanjani. Wekundu hao licha ya wachezaji wake kulipwa vizuri na kwa wakati tabu ipo kwenye suala la nidhamu.Wachezaji, baadhi yao hulewa, kuchelewa mazoezini, limekuwa likiwasumbua labda ni kutokana na jinsi walivyokuwa wanalelewa. Tabu nyingine iliyopo kwa timu hizi. Ni viongozi kuwaingilia benchi la ufundi na kuwapangia.Tatizo lililopo kwenye timu hizo kila mtu anajua na ni Kocha, akiona mchezaji fulani hajapangwa au ni mchezaji wake wanaingilia na kumpangia kocha ambaye hukaa na wachezaji mazoezini. Kwa mfano, Zahera wakati anaondoka Yanga alikiri kuingiliwa kwenye maamuzi yake na hata kwa upande wa Simba, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara alikiri kuwa kuna muda walikuwa wanamshauri kocha apange wachezaji fulani.Kwa kauli hizo inaonesha dhahiri bado benchi la ufundi linaingiliwa, kitendo ambacho ni lazima kitaleta mgongano kwa sababu kocha ana wachezaji wake na viongozi wana wachezaji wao. Jambo lingine ni namna mashabiki wa klabu hizo wanavyokosa uvumilivu. Yaani wanataka kuona Simba au Yanga inashinda mechi zote kitu ambacho kinaweza kuwezekana au kisiwezekane.Mashabiki wa timu hizo ni wa ajabu wanadhani wao ni bora kuliko wengine. Timu zao zikifungwa na klabu ndogo basi wanalalamika kana kwamba wameonewa wakati mchezo unachezwa uwanjani dakika 90.Ni watu wa kwanza kuwanyooshea vidole makocha na viongozi wao kwa sababu wamepoteza mechi moja na kupata sare moja pengine. Hawaamini mpira ni mchezo wa makosa ukikosea mwenzako anakuadhibu.Halafu imani yao kubwa mmoja akifungwa ndio furaha yao mwaka mzima, baada ya hapo mengine ndio yaendelee. Kama timu hizi zimeamua kujiendesha kisasa, basi ni lazima wakubali kuacha mambo mengine na kukubali mabadiliko ya kweli ili kuleta ushindani mkubwa sio tu kwenye ligi bali michuano ya kimataifa.
4
MAOMBI ya marejeo ya kupinga adhabu ya kunyongwa hadi kufa ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Christopher Bageni yamegonga mwamba baada ya Mahakama ya Rufaa kuyatupitia mbali.Kutokana na hali hiyo, mahakama hiyo imebariki adhabu ya kunyongwa hadi kufa, iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kufuatia mauaji ya wafanyabiashara wa madini wa Mahenge mkoani Morogoro.Wafanyabiashara waliouawa ni Sabinus Chigumbi na ndugu yake, Ephraim Chigumbi na mwenzao, Mathias Lunkombe na dereva teksi, Juma Ndugu, ambao Januari 14,2006 waliuawa kwa kupigwa risasi katika Msitu wa Pande uliopo wilayani Kinondoni, Dar es Salaam.Mwaka 2016 Bageni aliwasilisha maombi ya marejeo mahakamani hapo, akiomba mahakama hiyo ibadilishe uamuzi wake, uliotolewa na jopo la majaji watatu, Bernad Luanda, Sauda Mjasiri na Semistocles Kaijage, kufuatia rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), akipinga hukumu iliyomwachia huru yeye na wenzake nane.Akisoma maamuzi ya marejeo, Naibu Msajili Mwandamizi wa mahakama hiyo, Elizabeth Mkwizu alisema Bageni aliwasilisha sababu mbili za kupinga hukumu hiyo, ambazo ni kudai kunyimwa haki ya kusikilizwa na nyingine ni kulalamikia mahakama kumtia hatiani kwa kuzingatia ushahidi wa mshitakiwa mwenzake namba nne, Koplo Rajabu Bakari.Mkwizu alisema mrufani alidai wakati Mahakama ya Rufaa inaamua kuhusu rufaa iliyowasilishwa na DPP kuhusu kuachiwa kwa washitakiwa hao ilileta hoja mpya, ambazo hazikuwepo awali na hivyo waliangalia kwa makini hakukuwa na kipya walichokuwa wamefanya.
3
BAADHI ya wachambuzi na makocha wa soka nchini wametaja timu tano zinazoweza kufika mbali kwenye fainali za Mataifa ya Afrika zinazoendelea nchini Misri, huku wenyeji wakipewa asilimia 100.Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wachambuzi hao Ally Mayai, Dominick Salamba na Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ kila mmoja ameitaja Misri kuwa inaweza kufika mbali zaidi na hata kuchukua Kombe la Afrika. Kwa upande wa Mayai alisema sababu ya kuwapa nafasi wenyeji ni kutokana na historia iliyopita, ikionesha kuwa Misri iliwahi kuandaa michuano hiyo mara nne na mara tatu kombe likabakia kwao.Pia, alizitaja timu nyingine zenye nafasi kuwa ni Cameroon kwa kuwa wameanza vizuri na huenda wakataka kupambana ili kutetea taji walilolitwaa Gabon, huku akisema Algeria ina kikosi bora chenye uwezo, Ghana wana wachezaji wenye uzoefu na Morocco kwa sababu ina kocha aliyewahi kutwaa mataji mara tatu. “Kila timu ina ubora wake na yeyote anaweza kufanya makubwa kutokana na uzoefu wa wachezaji wao kwenye mashindano hayo,” alisema.Kocha wa zamani wa Simba, Mwadui na Dodoma FC, Julio alisema bado pana ugumu kwa sababu ndio kwanza mapema ila anaziona Misri, Algeria na Senegal katika jicho la mbali.Alisema timu nyingi ni bora na nyingine hubadilika kutoka mechi moja kwenda nyingine hivyo, ni kazi kutabiri mapema. Mchambuzi Salamba alisema michuano hiyo inaonekana migumu kutokana na mbinu za kiufundi kutofautiana ila anaipa nafasi Senegal kutokana na kuwepo kwa muunganiko bora wa kikosi chao.Pia, Nigeria kutokana na uwezo wa kumiliki mpira ingawa katika kasi ya kushambulia kwao sio kubwa, Cameroon kuwa wana vijana wenye kasi, Misri ikibebwa na uzoefu na ni wenyeji lakini pia, Algeria kutokana na kucheza mpira wa nguvu na wenye kasi. Nigeria juzi ndio ilikuwa timu ya kwanza kukata tiketi ya kucheza hatuia ya 16 bora kabla ya wenyeji Misri hawajaifuata baadae.
4
Matokeo ya uchaguzi wa urais nchini Kenya yameingia shubiri baada ya Mahakama Kuu nchini humo, kubatilisha ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta dhidi ya mpinzani wake mkuu Raila Odinga na kuamuru uchaguzi huo urudiwe ndani ya siku 60. Uamuzi huo umefikiwa leo Septemba 1, kutokana na maombi ya Odinga ambaye ni mgombea wa Muungano wa Upinzani NASA, ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8, mwaka huu, uliompa ushindi Rais Kenyatta. Katika maombi yake, Odinga alisema kura zake zilipunguzwa kwenye baadhi ya vituo na kuongezewa mpinzani wake, lakini kubwa zaidi ni kukiukwa kwa taratibu za uchaguzi ambapo baadhi ya fomu muhimu za matokeo ya uchaguzi kama vile fomu namba 34A, B na C, hazikupatikana siku ya kutangazwa kwa matokeo. Katika shauri hilo, majaji wanne kati ya sita, wamekubaliana kuwa Tume Huru ya Uchaguzi  (IEBC), imeshindwa kusimamia vema uchaguzi huo na hivyo kusababisha kasoro kadhaa kwenda kinyume na katiba ya Kenya. Pamoja na mambo mengine, akizungumza baada ya uamuzi huo wa mahakama Odinga amesema NASA itawashtaki maofisa wa tume kwa kufanya uhalifu mkubwa kwa nchi hiyo. Baada ya uamuzi huo kutolewa, baadhi ya wafuasi wa Odinga walionekana kufurahi kwa kuimba mapambio huku wale wa Kenyatta wakizimia na wengine kuongea kwa hasira kama ishara ya kupinga uamuzi huo wa mahakama.
2
  Na CHRISTOPHER MSEKENA, WIKI hii uongozi wa kituo cha runinga cha MTV Base kinachoandaa Tuzo za MTV Africa Music Awards (MTV MAMA 2016) kilitangaza majina ya mastaa wa muziki Afrika ambao wameingia kwenye kinyang’anyiro cha tuzo hizo mwaka huu. Tuzo hizo kubwa zenye heshima ya aina yake Afrika huwa zinavuka mipaka ya bara hili na kuwasogeza karibu wasanii wakubwa kutoka  mabara mengine kama vile Marekani na Ulaya na mwaka huu mastaa kama Drake, Beyonce, Adele, Future na Rihana wamekutanishwa kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kimataifa. Sherehe za utolewaji wa tuzo hizi zinatarajiwa kufanyika huko Johannesburg, Afrika Kusini, Oktoba 22, mwaka huu na burudani juu ya jukwaani itasimamiwa na Patoranking, Kwesta, Diamond Platnumz, Emtee, Ali Kiba, Cassper Nyovest na Ycee. Kama kawaida Bongo Fleva haipo nyuma ambapo mwaka huu wasanii wake watatu wameingia kwenye kinyang’anyiro cha tuzo hizo. Hao si wengine bali ni Ali Kiba, Navy Kenzo na Diamond Platnumz. Kiba, ambaye pia atatumbuiza yupo kwenye kipengele cha Wimbo Bora wa Kushirikiana (Best Collaboration) kupitia wimbo alioshirikiana na Kundi la Sauti Sol unaoitwa Unconditionally Bae, tuzo inayowaniwa na wasanii wengine kama vile AKA, Nasty C, Patoranking na DJ Maphorisa. Kwa mara ya kwanza kundi linaloundwa na wapenzi, Aika na Nahreel limeendelea kudhihirisha ubora wake kwani safari hii limeweza kupenya na kuingia kwenye tuzo hizi zenye ushindani mkubwa. Kundi hilo linalofanya poa na ngoma yake ‘Kamatia Chini’ lipo kwenye Kipengele cha Kundi Bora (Best Group). Tuzo hii pia ina ushindani wa aina yake kwa sababu inayakutanisha makundi mengine yaliyofanya vizuri mwaka huu. Makundi kama Micasa, Toofan, R2bees na Sauti Sol yanaweza kuwapa changamoto Navy Kenzo, ila kura yako wewe shabiki wa Bongo Fleva inaweza ikafanya maajabu, Navy Kenzo wakaondoka na tuzo hiyo mwaka huu. Mbali na Navy Kenzo na Ali Kiba kuwania tuzo hizi, tena ikiwa ni mara yake ya pili kuingia kwenye tuzo hizo, big boss wa WCB, Diamond Platnumz mbali na kutumbuiza ana changamoto ya kuviruka vizingiti vya mastaa wengine waliopo kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kiume (Best Male). Achana na kina AKA, Patoranking na Wizkid ambao ni levo yake na anawamudu, kuna kigingi kingine cha kahawa nyeusi au Dj Black Coffee ambacho ni kikongwe na cha kuogopwa kwenye tuzo hii kulingana na sifa zake kwenye muziki wa Afrika. Hii inakuwa mara ya pili kwa Diamond kukutana na Black Coffee. Nadhani unakumbuka jina la mchezeshaji huyu wa muziki lilivyokua ghafla kwenye masikio ya mashabiki pale ambapo Diamond alitoka jasho bila mafanikio kwenye tuzo za Black Entertaiment (BET) zilizofanyika Los Angeles, Marekani mwezi Juni, mwaka huu. Dj Black Coffee ambaye ni mlemavu wa mkono wa kushoto aligeuka kuwa mada inayozungumzwa zaidi na Watanzania hasa kwa wale  ambao waliweka matumaini ya ushindi Diamond, Wizkid, Yemi Alade, AKA, MzVee, Cassper Nyovest na Serge. Ukanda wa Afrika Mashariki ulikuwa haumfahamu sana Dj Black Coffee ila ushindi wake uliochangiwa na kushindwa kwa Diamond aliyekuwa anaiwakilisha Afrika Mashariki basi alifanikiwa kujizolea mashabiki wa kutosha. Lakini kabla kidonda cha kuikosa tuzo ya BET hakijapona sawasawa, Diamond  anakutana tena na Dj huyu. Je, anaweza kuchomoka na tuzo au atabanwa mbavu? Kama kigezo kikiwa ni wingi wa kura na wewe Mtanzania ukipiga kura kwa wingi basi  Diamond na washiriki wengine kutoka Tanzania wataweza kuibuka na tuzo hizo. Piga kura sana kwa ajili yao; Diamond, Ali Kiba na Navy Kenzo. Kila la kheri mashujaa wetu.
1
Mbali na kutozwa faini pia TRA imepanga kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara ambao hawatafika katika ofisi za Mamlaka hiyo kuandikisha biashara zao.Meneja wa TRA Wilaya za Hai na Siha, Sylver Rutagwelera, alisema hayo hivi karibuni na kufafanua kuwa Sheria ya kodi ya mapato ya 2004, imeitaka Serikali kutoa siku 90 kila unapoanza mwaka wa kalenda, ili kuwapa muda walipakodi kutangaza mapato yao na kulipa kodi zao kwa hiari.“Aprili mosi mwaka huu, siku 90 za hiari zikipita, sheria itatumika kwa wale ambao watakaidi kulipa kodi kwa wakati na ambao watakuwa hawajatangaza mapato ya biashara zao watalazimika kulipa faini,” alisema Rutagwelera.Rutagwelera alisema wafanyabiashara wote wanatakiwa kufika katika ofisi za TRA kuandikisha biashara zao ili wapatiwe namba ya biashara (TIN) bila kujali analipa kodi au halipi kodi.Lengo la TRA kwa mujibu wa Rutagwelera, ni kuendelea kuboresha ulipaji kodi kwa kutumia mfumo mpya wa kutoa risiti kwa kutumia mashine maalum zinazotolewa na mamlaka hiyo na kuwataka wafanyabiashara watambue kuwa suala la ulipaji wa kodi ni wajibu kwa maendeleo ya Taifa na Watanzania wote kwa ujumla.“Ulipaji mpya wa kodi kwa kutumia mashine maalum za kutolea risiti (EFDs), unaonekana kupingwa na baadhi ya wafanyabiashara, nataka niseme kwamba Serikali haitaondoa mfumo huu bali adhabu kali itachukuliwa kwa kila mfanyabiashara atakayekiuka.Majembe yetu yapo na yatafanya kazi yake kwa uadilifu kwa wale ambao si waadilifu,” aliongeza.Aliwataka wafanyabiashara kutambua kuwa mashine za utoaji wa risiti hazitasaidia tu Serikali katika kukusanya mapato bali pia zitamsaidia mfanyabiashara kutunza kumbu kumbu na kuepuka kuibiwa na wafanyakazi wao wasio waaminifu.
5
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imeutaka upande wa utetezi kufuatilia taarifa za ugonjwa wa mshitakiwa wa tatu ambaye ni Ofi sa Usafi rishaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), George Ntalima kwa maofi sa Magereza kutokana na kutofi ka mahakamani mara ya pili.Hatua hiyo imekuja baada ya Wakili wa Serikali Mwanzamizi, Ladslaus Komanya kudai mbele ya Hakimu Mkazi, Salum Ally kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya washitakiwa kusomwa maelezo ya awali.Alidai mshitakiwa wa tatu hayupo mahakamani hivyo, alimtaka wakili wa mshitakiwa kuieleza mahakama alipo mteja wake. Wakili wa Ntalima, Tuli Kaundime alidai mshitakiwa huyo ni mgonjwa kwani anasumbuliwa na majipu yaliyosababisha homa kali na ndio sababu ya kushindwa kufika mahakamani. Alidai afya ya mshitakiwa huyo imedhorota hivyo aliomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.Wakili Komanya alidai wakili wa mshitakiwa alitakiwa kutoa taarifa huyo huku ikiambatanishwa na taarifa rasmi kutoka magereza ili ijulikane kama anapatiwa matibabu au amepumzishwa.Alidai kwa ajili ya kutenda haki kwa washitakiwa wengine wakili huyo alete uthibitisho juu ya ugonjwa na sababu za kutompeleka mahakamani. Akijibu hoja hiyo, Kaundime alidai mteja wake yupo mahabusu chini ya uangalizi wa magereza hivyo, si sahihi yeye kupeleka taarifa za ugonjwa au kueleza alipo mshitakiwa wakati wanafahamu yupo kwenye mikono salama ya magereza.Alidai wanaopaswa kutoa taarifa hiyo ni magereza. Baada ya kueleza hayo, Hakimu Ally alisema ni wajibu wa upande wa mashitaka kupata taarifa za mshitakiwa huyo kutoka magereza. Hata hivyo, aliutaka upande wa mashitaka kuwasiliana na magereza ili kupata taarifa za mshitakiwa huyo na kuieleza mahakama maendeleo yake. Hakimu Ally aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 19, mwaka huu kwa ajili ya kuwasomea washitakiwa maelezo ya awali.Mbali na Ntalima, washitakiwa wengine katika kesi ya uhujumu uchumi wengine ni aliyekuwa Mkurugenzi wa NIDA, Dickson Maimu, Meneja Biashara wa NIDA, Avelin Momburi; Ofisa Usafirishaji, George Ntalima; Xavery Silverius maarufu kama Silverius Kayombo na Mkurugenzi wa Sheria NIDA, Sabina Raymond. Maimu na wenzake wanakabiliwa na mashitaka 55 yakiwamo ya kutakatisha fedha na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 1.175.Kati ya mashtaka mapya 55 waliosomewa washitakiwa hao, yapo ya kuisabishia serikali hasara ya Sh bilioni 1.175 ; utakatishaji fedha; kughushi; kuwasilisha nyaraka za uongo ili kumdanganya mwajiri wao; kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu; matumizi mabaya ya madaraka na kuongoza genge la uhalifu. Hata hivyo, Maimu, Ntalima na Silverius wamerudishwa rumande kutokana na mashitaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili kutokuwa na dhamana huku Momburi na Raymond wakiwa nje kwa dhamana.
3
NA PETER FABIAN, MWANZA KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro, amesema mfungwa mmoja na mahabusu wawili wameuawa baada ya kutoroka gereza kuu la Butimba jijini Mwanza. Alisema mahabusu hao, walifariki dunia wakiwa hospitali baada ya kipigo cha wananchi waliowakamata huku mfungwa akifariki baada ya kupigwa risasi na askari alipojaribu kutoroka alipokuwa akienda kuonyesha dereva teksi aliyekuwa awasaidia kuondoka Mwanza endapo wangefanikiwa kutoroka gerezani. Kamanda Muliro, alisema mfungwa aliyeuawa ni ni namba 200/2019 George Aloyce (34) ambaye alikuwa anatumikia kifungo cha miaka 15 katika gereza hilo kwa kosa la uhujumu uchumi ambaye alikula njama na kuwashawishi mahabusu wawili ili waweze kutoroka.  Alisema mahabusu wawili ambao pia waliuawa, walikuwa wanakabiliwa na kesi ya mauaji jijini Mwanza ambao kwa pamoja walifanikiwa kutoroka gereza la kuu la Butimba April 14, mwaka huu 12:30 jioni.  “Mfungwa huyu (Aloyce) alifanikiwa kuwashawishi mahabusu namba 3444/2016 Yusufu Benard (34) aliyekuwa na kesi ya mauaji na mahabusu namba 1177/2017, Seleman Seif (28) aliyekuwa akikabiliwa pia na kesi ya mauaji katika moja ya msikiti jijini Mwanza kutoroka kutoka ndani ya ngome ya gereza kuu,”alisema. Alisema baada ya kuonekana wanakimbia, askari Magereza walipiga filimbi, huku wakiwakimbiza watuhumiwa hao ambapo pia wanananchi wanaoishi jirani na gereza hilo waliitikia na kuanza kuwakimbiza na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wote watatu. “Walipowakamata walianza kuwapa kipigo kikali na baada ya askari Magereza na polisi kufika wananchi waliwakabidhi ili kuondoka nao, lakini hali zao zilikuwa mbaya kutokana na kipigo walichopata kutoka kwa wananchi,”alisema. Kamanda alieleza polisi kwa kushirikiana na Magereza, waliwachukua na kuwapeleka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure Mwanza ili wapatiwe matibabu, lakini hali ya mahabusu Yusuf Benard na Seleman Seif ilibadilika wakati wakipatiwa matibabu na walifariki dunia. “Mfungwa George Aloyce alipotibiwa na kuruhusiwa aliomba kwa askari polisi awapeleke eneo la mabatini kwa dereva wa teksi ambaye alidai  angewasafirisha kwenda mji mdogo wa Katoro wilayani Geita, baada ya kufanikiwa kutoroka gerezani,”alieleza. Kamanda alisema walipofika Mabatini akiwa chini ya ulinzi wa polisi akiwa amefungwa pingu, aliomba afunguliwe ili dereva aliyetaka kuwaonyesha asione kama bado kafungwa. Alisema licha ya askari kukata ombi lake hilo, bado aliifanikiwa kuwakimbia polisi ambao walimkimbiza. “Mtuhumiwa alipokimbia na askari polisi walimtaka asimame ,huku wakipiga risasi hewani, alikataa kutii amri ndipo polisi wakampiga risasi za miguu na kumkamata lakini walipokuwa wakimpeleka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure alifariki dunia njiani,”alisema. Kamanda alitoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na kuwawashukuru wananchi waliojitolea na kushirikiana na askari wanawakamata watuhumiwa hao baada ya kutoroka gerezani.
3
WEKUNDU wa Msimbazi, Simba leo watakuwa ugenini jijini Arusha dhidi ya African Lyon katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.Kocha wa Simba Patrick Aussems amesema, atawapumzisha baadhi ya wachezaji waliocheza dhidi ya Yanga ili wawe fiti kwa mechi ijayo dhidi ya Azam FC.Simba itaingia kwenye mechi hiyo ikiwa na morali ya hali ya juu baada ya kumfunga mtani wake wa jadi, Yanga bao 1-0 katika mchezo mwingine wa ligi hiyo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa mwishoni mwa wiki iliyopita.Simba na Lyon zinapokutana hupambana, kila mmoja akionesha ubora wake kumkazia mwenzake. Wekundu hao hawataisahau Lyon aliwahi kuwaharibia rekodi msimu wa mwaka juzi kwa kupigwa 1-0 kwenye uwanja wa Uhuru, baada ya kucheza michezo karibu 13 bila kupoteza.Lakini kwa kipindi kile Simba haikuwa na kikosi bora kama cha sasa, wanaonekana kiufundi wako vizuri zaidi ukilinganisha na Lyon ambao wako kwenye wakati mgumu wa kutaka kushuka daraja.Mechi ya leo ni kiporo cha raundi ya kwanza kwa Simba huku Lyon ikicheza mechi yake ya mzunguko wa pili, mechi ya kwanza mabingwa watetezi Simba waliibuka na ushindi wa mabao 2-1.Mpaka sasa Simba imecheza michezo 16, imeshinda 12, sare tatu na kupoteza mchezo mmoja ikiwa na pointi 39. Lyon imecheza michezo 26, imeshinda minne, sare tisa na kupoteza 13 ikishika mkia kwa pointi 21.Bila shaka hautakuwa mchezo rahisi kwa kila mmoja, Simba inahitaji pointi tatu kuendeleza rekodi yake ya ushindi na kuwa katika nafasi nzuri ya kutetea taji na Lyon inahitaji kupambana kupata pointi tatu ili kujinusuru katika ukanda wa kushuka daraja.Lyon itakuwa na kazi kubwa ya kuwazuia washambuaji hatari wa Simba akiwemo Meddie Kagere mwenye mabao tisa, Emmanuel Okwi na John Bocco kila mmoja akiwa na mabao saba.Si hao tu kuna mchezaji hatari kama Zana Coulibaly ambaye mara nyingi amekuwa akipandisha mashambulizi na kutengeneza krosi za hatari na hata kuingia eneo la kufunga.Kocha wa Simba, Patrick Aussems alisema muhimu katika mchezo huo ni pointi tatu ingawa anaona kuna changamoto ya uwanja kutokuwa imara.“Changamoto ninayoiona ni uwanja lakini tutakabiliana nao kupata kile tunachokitaka,” alisema na kuongeza kuwa anatarajia kuwapa nafasi wachezaji wote na kuwapumzisha wengine kutokana na ugumu wa ratiba.Alisema anatarajia mashabiki wengi watajitokeza kwani anaamini kila mkoa wanaoenda wako wengi na kuwaahidi kuwapa raha. Mchezaji wa African Lyon, Jabir Aziz alisema wamejipanga vizuri kuwakabili Simba lengo lao ni kuhakikisha wanafanya vizuri.“Tunaingia tukiwaheshimu wapinzani wetu ni wazuri na ndio wawakilishi wetu wa nchi kwenye michuano ya kimataifa, tumejipanga kupambana nao lengo letu ni pointi tatu,” alisema.
4
Sasa ni rasmi kuwa aliyekuwa kiungo wa ulinzi wa Simba James Kotei, amesajiliwa na klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa kandarasi ya miaka mitatu. Msimu uliopita Kaizer Chiefs wamemaliza katika nafasi ya 9, hivyo wameamua kusajili wachezaji wenye uzoefu wa mechi za kimataifa ili kurudi katika ubora wao msimu ujao. Taarifa rasmi kutoka ukurasa wa Twitter wa klabu hiyo imethibitisha kuwa Kotei ambaye ni raia wa Ghana atakuwa na timu hiyo msimu ujao. Kotei alisajiliwa na Simba Desemba 2016, muda mfupi baada ya kufanya majaribio ya kujiunga na kikosi cha Simba na kufuzu. Kotei ambaye aliisaidia Simba kwenye Ligi nya Mabingwa Afrika msimu uliopita ilipofika robo fainali, alichaguliwa kuwa kiungo bora kwenye tuzo za Mo Simba Awards. Mpaka sasa haijawekwa wazi ni kiasi gani Simba wamevuna kwenye usajili huo kutokana na kumuuza Kotei ambaye alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja. Player Updates: Chiefs confirm Kotei! Kaizer Chiefs have signed James Agyekum Kotei on a three-year contract. The 25-year-old defensive midfielder hails from Ghana. He joins Amakhosi from Simba Sport Club in the Tanzanian Premier League. #Amakhosi4Life pic.twitter.com/2ws82kIAmg — Kaizer Chiefs (@KaizerChiefs) June 26, 2019
4
THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa Azam, Aristica Cioaba, ameendelea kukiweka fiti kikosi chake kuhakikisha kinakuwa na moto wa kuotea mbali katika mechi zao za Ligi Kuu Tanzania Bara. Azam waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Biashara United katika mchezo wao wa mwisho wa ligi hiyo kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam. Ushindi huo walipata wakiwa wametoka kupoteza mechi mbili mfululizo, wakifungwa bao 1-0 na Simba pamoja na Ruvu Shooting. Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Jafar Iddy, alisema baada ya kumaliza mchezo wao wa mwisho dhidi ya Biashara United, benchi la ufundi liliongeza zaidi mazoezi katika kipindi hiki ambacho ligi imesimama kupisha mechi za kimataifa. “Wachezaji wanaendelea na mazoezi ikiwa ni maandalizi ya mechi ambazo zinatukabili mbele yetu, ligi imesimama hivyo huu utakuwa muda mzuri kwa sisi kujiandaa vizuri kwa ajili ya michezo inayotukabili,” alisema. Alisema Cioaba anautumia muda huu kuhakikisha wachezaji ambao hawajaenda kwenye timu zao za Taifa, wanakuwa fiti na kuyafanyia kazi baadhi ya makosa. Idd alisema kwa sasa wanaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Azam Complex na kwamba hawana mchezaji ambaye ni majeruhi. 
4
MENEJA wa Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Diana Masalla, amesema mwananchi yeyote atakayefi chua wakwepa kodi na TRA ikafuatilia na ikagundulika ni kweli na ikakusanywa, atalipwa asilimia tatu ya kodi iliyokusanywa lakini haitazidi Sh milioni 20.Aliyasema hayo wakati wa Jukwaa la Biashara na Uchumi lililofanyika katika wilaya ya Busega, mkoani Simiyu, ambalo lengo lake ni kujadili fursa, changamoto na kero mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara na wawekezaji wilayani humo na kuzitafutia ufumbuzi.“Natoa wito kwa wananchi na washiriki wa jukwaa hili kuwafichua wakwepa kodi wote kwa sababu watu hao wanaiibia serikali yetu mapato na wanarudisha nyumba jitihada za serikali za kuwaletea maendeleo wananchi,” alisema.Aidha, Masalla aliwahimiza wafanyabiashara na wawekezaji walioshiriki jukwaa hilo kuhakikisha wanatoa taarifa wanapofunga biashara kutokana na sababu mbalimbali ili kuepuka kuendelea kutozwa kodi au kuonekana wamekaidi kulipa.“Ni muhimu kutoa taarifa TRA pale ambapo mfanyabiashara amefunga biashara yake, lakini pale anapofungua ni muhimu pia kuitaarifu TRA ili kuepuka kuendelea kutozwa kodi unapofunga biashara na pia kuanza kutozwa kodi sahihi pale unapofungua biashara,” alisisitiza Masalla.Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Wilaya ya Busega, David Mateko, alimpongeza meneja wa TRA mkoa wa Simuyu kwa kutoa elimu ya kodi kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiashara pamoja na mkuu wa wilaya hiyo kwa kuwahamasisha.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewapokea watalii 330 wakiwemo wafanyabiashara na wawekezaji kutoka jimbo la Zhejiang, China ambao waliwasili juzi usiku kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).Watalii hao ni kundi la kwanza miongoni mwa watalii 10,000 ambao wanatarajiwa kutembelea Tanzania mwaka huu, chini ya mpango unaosimamiwa baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Bodi ya Utalii Tanzania na kampuni ya TouchRoad International Holding Group ya China.Akizungumza na watalii hao kwenye chakula cha jioni kilichoandaliwa kwenye Hoteli ya Mount Meru juzi usiku, Waziri Mkuu Majaliwa alimshukuru Mwenyekiti wa Kampuni ya Touchroad Group, Liehui He kwa kuwaunganisha Watanzania na Wachina kupitia mpango wake wa kukuza utalii.“Mbali na kutuunganisha Watanzania na Wachina, tunakushukuru pia kwa kuamua kuitangaza Tanzania kuwa nchi yenye fursa nyingi za kitalii duniani,” alisema.Waziri Mkuu alitaja vivutio vingine vilivyopo ambavyo watalii hao wanaweza kuvifurahia kuwa ni mbuga za Ngorongoro, Serengeti, Manyara, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Katavi na akawataka waende visiwa vya Zanzibar kuona fukwe zenye mchanga mweupe na kupata marashi ya karafuu.Aliwapongeza watendaji wa Bodi ya Utalii na makampuni ya utalii kwa maandalizi na mapokezi mazuri kwa watalii hao.Pia alimpongeza Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kushirikiana na TouchRoad na kuifanya Tanzania ipokee watalii wengi.Akielezea ujio wa kundi la kwanza la watalii, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini, Devotha Mdachi alisema watalii hao wametokea Djibouti ambako walikaa kwa siku moja, na hapa nchini watakaa kwa siku nne na kisha wataelekea Bulawayo, Zimbabwe ambako watakaa kwa siku mbili na kurejea China.Mapema, akizungumza katika mkutanohuo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi alisema ujio wa watalii hao ni sehemu ya mpango mkubwa wa nchi wa kuongeza watalii kutoka China unaofahamika kama Tour Africa - The New Horizon.Aliwataka Watanzania wachangamkie fursa ya ujio wa wageni ili waweze kunufaika kiuchumi.“Naomba niwasihi Watanzania, hii ni fursa hatuna budi kuichangamkia ili wao wafurahie utalii nchini lakini nasi tunufaike na uwepo wao.”
5
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya,  alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele.  “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema
5
Na ADAM MKWEPU-DAR ES SALAAM SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeandika barua kwa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kudai pointi tatu za mchezo wa marudiano kati ya Serengeti Boys na Congo Brazzaville. TFF inadai pointi hizo baada ya Congo kumchezesha mchezaji Langa Lesse Bercy anayedaiwa kuzidi umri katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, kilichovaana na Serengeti Boys. Katika mchezo wa marudiano, Congo ilishinda bao 1-0 lililofungwa na Bercy na kufanikiwa kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Vijana zitakazofanyika mwakani nchini Madagascar, baada ya awali kufungwa mabao 3-2 ugenini. Mchezaji huyo alitakiwa kuwasili nchini Misri Novemba 19, mwaka huu ili kufanyiwa vipimo vya uchunguzi kuhusu umri wake, lakini inadaiwa alishindwa kufika kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake. Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas, alisema barua ya kudai pointi tatu ilitumwa juzi, baada ya kugundua makosa ya wapinzani wao ya kumchezesha mchezaji huyo aliyezidi umri unaotakiwa na CAF. Alisema TFF inatarajia kujibiwa barua hiyo ndani ya siku mbili, ambapo kama  CAF itaridhia na kuinyang’anya pointi Congo, Serengeti Boys itakata tiketi ya kucheza fainali za mwakani. “Tunafuatilia jambo hili kwa umakini wa hali ya juu maana kuna kila dalili ya wapinzani wetu kupokonywa pointi, hivyo tunasubiri majibu ya CAF baada ya siku mbili,” alisema Lucas. Kwa mujibu wa kanuni za CAF, udanganyifu wa umri ni kosa ambalo linaweza kupelekea nchi husika kufungiwa kushiriki mashindano husika kwa muda wa miaka mitatu.
4
NA OSCAR ASSENGA-TANGA WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage,  amefichua siri ya kufa kwa viwanda nchini mkoani Tanga, kutokana na ushindani usio sawa hasa kwa bidhaa zinazoingizwa kwa njia ya magendo hali iliyosababisha kukosa masoko. Amesema kitendo hicho cha kuingiza bidhaa kwa njia za magendo ni sawa na uhaini, ugaidi ambao unapaswa kushughulikiwa na wadau wote wa maendeleo ili kuweza kuutokomeza. Kauli hiyo aliitoa jana jijini Tanga, wakati akifungua maonesho ya biashara ya Kimataifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwahako na kuhusisha wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi. Alisema suala hilo linapaswa kuwekewa mipango mizuri ya kuhakikisha linatokomezwa ili kuweza kuendana na sera ya viwanda ambayo itakuwa ni muhimili muhimu wa kufungua uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kufikia kipato cha dola 3000. “Bidhaa nyingi zinaingizwa kwa njia ya magendo sana na hivyo kus+ababisha soko la bidhaa za ndani kushuka na huu ni sawa na uhaini na ugaidi kwa sababu bidhaa za magendo halizipiwi ushuru na madhara yake ni makubwa sana kwa ukuaji wa uchumi.  “Kutokana na hilo niwaagize viongozi wa mkoa huu akiwemo RC (Mkuu wa Mkoa) na wakurugenzi kuhakikisha bidhaa za magendo haziingia nchini kwani madhara yake ni makubwa kwa Taifa,” alisema Alisema madhara ya bidhaa za magendo inachangia kuua viwanda vya ndani na kuingiza sokoni bidhaa ambazo sio salama kwa matumizi. “Kama tunazibiti magaidi wanaweza kuweka sumu kwenye biashara za magendo na zitakapowafikia watanzania watakula na kupoteza maisha hivyo hakikisheni mnapiga vita biashara za magendo na tumieni bidhaa zilizotibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS),” alisema Waziri Mwijage. Awali akizungumza  katika kongamano hilo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella  alisema mkoa huo una utaratibu wa kujenga uhusiano kwa wananchi, wawekezaji na uwezeshaji kama moja ya eneo muhimu la kulinda na kukuza masoko.
3
WATU wawili wanaodaiwa kuwa majambazi wamefariki dunia kwa kupigwa risasi na wenzao, baada ya kutaka kuwatoroka askari wakati wa operesheni ya kuwasaka majambazi mkoani Shinyanga.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Saimon Haule alithibitisha hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari. Alieleza kuwa mauaji hayo yalitokea juzi saa 3:00 usiku katika vichaka vya Mtaa wa Buhangija Kata ya Ibinzamata Manispaa ya Shinyanga. Kamanda aliwataja waliouawa ni Geoffrey Ntabazi (29) na Ramadhani Masoud (33), ambao walikuwa wahusika kwenye matukio ya unyang'anyi na uvunjaji ya Januari 28 na 30, mwaka huu.Kamanda Haule alisema watu hao wanaodaiwa kuwa ni majambazi, walikufa kwa kupigwa risasi na majambazi wenzao, baada ya kutaka kuwatoroka wakati wa operesheni ya kuwasaka majambazi waliotajwa na marehemu hao kuhusika kwenye matukio ya unyang'anyi na uvunjaji.Alisema majambazi hao walitaja silaha ambayo huitumia pamoja na wenzao, waliokuwa wamejificha kwenye vichaka eneo la Buhangija. Baada ya kufika hapo, ghafla majambazi hao waliokuwa wamejificha, walianza kuwashambulia askari na kumpata jambazi mmoja na mwingine aliyekuwa ameongozana na askari.
3
Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM FAMILIA ya Buhela na Hilda mwaka 2013 ilijaliwa kupata mtoto wa kiume waliyemuita Apulihe. Apulihe ni jina la asili la watu wa Mkoa wa Njombe likimaanisha ‘Mungu amesikia’ au kwa kiingereza ‘Godlisten’. Kuzaliwa kwa mtoto huyo kuliongeza furaha na upendo ndani ya familia hiyo kama ambavyo huwa ni matarajio ya wanandoa walio wengi. Hilda ambaye pia ni Katibu wa Chama cha wazazi walio na watoto wenye tatizo la usikivu, anasema aliamua kumuita jina hilo mtoto wake huyo baada ya Mwenyezi Mungu kusikia kilio chake. “Huyu ni mtoto wangu wa tatu, kila nikibeba ujauzito nilikuwa napata misukosuko mingi, mimba zilikuwa zinanisumbua hali iliyosababusha nilazwe ‘bedrest’. Lakini hali ilikuwa tofauti kwa Apulihe, sikuumwa kabisa hivyo nikaona Mungu amesikia kilio changu, ndio maana alipozaliwa nikachagua kumuita jina hilo,” anasema. Anasema maendeleo ya ukuaji wa mtoto wake huyo yalikuwa mazuri lakini kadiri muda ulivyokuwa ukizidi kwenda mbele alibaini kasoro kadhaa zilizompa wasiwasi mwingi. “Alikuwa na afya nzuri na hata nilipompeleka kliniki madaktari walikuwa wakinipongeza kila wanapompima na kuona kuwa anaendelea vizuri, lakini mwanangu alikuwa tofauti na watoto wengine, alikuwa hawezi kutoa sauti,” anasema. Anasema Apulihe alipofikisha umri wa miaka miwili alikuwa bado hajaanza kutamka neno baba au mama kama ambavyo watoto wengi wa umri wake hutamka. “Hali hii ilizidi kuniongezea wasiwasi niliokuwa nao, kusema ukweli kama mama nilitamani mwanangu aweze kutamka maneno hayo kama ilivyokuwa kwa watoto wengine, lakini hakuweza,” anasema. Safari ya matibabu Anasema aliwashirikisha watu wa karibu na familia yake juu ya suala hilo ambapo walimshauri kwenda katika nchi moja iliyopo kwenye Ukanda wa Afrika Mashariki kwani ndipo ambako angeweza kupata matibabu. “Waliniambia kuwa mwanangu atakuwa anasumbuliwa na tatizo la usikivu, nikasafiri hadi kwenye hiyo nchi, wakamfanyia kipimo kiitwacho ABR na kweli walikuta anasumbuliwa na tatizo hilo la usikivu, nilitumia zaidi ya Sh milioni tisa. “Lakini jambo lililonikatisha tamaa ni pale daktari wa hospitali ile aliponieleza kuwa hakuna matibabu ambayo mwanangu anaweza kupatiwa ili kumsaidia dhidi ya tatizo hilo,” anasema. Hilda anasema baada ya kuyapokea majibu hayo alirejea nchini kwa huzuni kubwa. “Lakini sikukata tamaa, nikawa naendelea kusoma kwenye mitandao mbalimbali kuhusu tatizo hilo, jinsi linavyotokea na iwapo kama linatibika. Nikiwa katika mchakato huo kuna mtu alinishauri nimlete hapa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwani kuna madaktari bingwa. “Nilifunga safari nikaja hadi Muhimbili, nikaonana na madaktari na kuwaeleza jinsi ilivyo na wao wakanieleza kuwa tatizo hilo linatibika, huo ulikuwa mwanzo wa kurejea upya kwa furaha yangu,” anasema. Rufaa ya India Hilda anasema ilipofika Desemba 7 mwaka 2012, mtoto wake alipata bahati ya kuwa miongoni mwa watoto waliopewa rufaa na serikali kwenda nchini India kufanyiwa matibabu ya kupandikizwa vifaa vya usikivu ‘cochlea implant’. “Walimfanyia upasuaji Desemba 26 mwaka 2012, baada ya kupandikizwa kifaa hicho nilianza kumuongelesha nikijua kuwa tayari atakuwa ananisikia kumbe si hivyo. Kwa kuwa hii ni mashine ambayo ipo ‘programed’ hadi ifikie hatua ya kuwashwa ili aweze kusikia kama watu wengine huwa ni hatua inayochukua muda mrefu kidogo, madaktari walinieleza. “Nilivumilia hadi ilipofika Januari 5, 2013 ambapo waliiwasha rasmi, kwa kweli hata baada ya kuwashwa ilichukua tena muda kidogo hadi alipoweza kuongea, ilikuwa rahisi kwake kujifunza kwani ulikuwa umri mwafaka wa kujifunza lugha kwa mtoto wa umri wake,” anasema. Kisa kingine Vivian Vicent ni mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na nusu sasa, naye amezaliwa na tatizo la usikivu. Lucy Kizaa ambaye ni mama wa mtoto huyo anasema wao ni wakazi wa Chunya, mkoani Mbeya na kwamba tatizo hilo liligundulika akiwa na umri wa miezi mitatu. “Alikuwa anashindwa kulia vizuri kama watoto wengine wa umri wake, alipolia alikuwa kama anajikakamua kutoa sauti, nikaamua kumpeleka katika Zahanati moja iliyopo eneo la Chunya,” anasema Kizaa. Anasema baada ya madaktari kumfanyia vipimo hawakugundua tatizo lililokuwa likimsumbua hivyo walimshauri kumfikisha katika hospitali kubwa kwa uchunguzi zaidi. “Nilimpeleka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ambapo walimfanyia vipimo lakini nao hawakugundua tatizo hivyo walimpatia rufaa ya kuja hapa Muhimbili, baada ya kufanyiwa vipimo ndipo akagundulika kuwa na tatizo la usikivu,” anasema. Anasema Vivian alipewa rufaa ya kwenda India Machi 2014, ambapo alifanyiwa upasuaji wa kuwekewa ‘cochlea implant’ na sasa ameanza kujifunza lugha ili aweze kuwasiliana. Daktari Mkuu wa Kitengo cha Masikio, Pua na Koo wa Muhimbili, Dk. Edwin Liyombo, anasema idadi ya watoto wanaozaliwa na tatizo la usikivu nchini inazidi kuongezeka kadiri miaka inavyosogea mbele. “Kitengo hiki kilianza mwaka 2003 wakati huo katika kliniki yetu tulikuwa tukihudumia watoto watatu kwa wiki lakini hadi kufikia mwaka huu idadi imeongezeka ambapo kwa wiki tunaona watoto 16,” anasema. Anasema tangu mwaka 2003 hadi sasa tayari watoto 45 wamefanyiwa upasuaji wa kupandikizwa kifaa cha kuwezesha usikivu ambacho kitaalamu kinaitwa ‘cochlea implant’. Sababu za ukiziwi Daktari huyo anasema zipo nyingi ikiwamo matumizi holela ya dawa zenye kemikali kali kama Quinine ambayo hutumika kutibu ugonjwa wa malaria na ile ya gentamacin inayotumika kutibu ugonjwa wa UTI. “Hatari zaidi hujitokeza pale mjamzito anapotumia dawa hizo bila kufuata ushauri wa daktari, akizidisha kipimo cha dozi anayopaswa kunywa hali hiyo huchangia kwa asilimia kubwa mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la usikivu (kiziwi),”anasema Dk. Liyombo. Anasema ndiyo maana wataalamu wa afya huwa wanawashauri wajawazito kuhudhuria kliniki kila wakati na kufuata ushauri wanaowapatia. “Quinine na Gentamacin ni mfano tu wa dawa ambazo huchangia kuchochea mtoto kupata tatizo la usikivu lakini zipo nyingi, sasa matumizi holela ya dawa zenye sumu, dozi inapozidishwa sumu hizo huenda kuua seli zilizoko ndani ya sikio katika eneo la ‘Cochlea’,” anasema. Anasema seli hizo zinapokufa sikio hushindwa kupokea mawimbi ya sauti na kwa kuwa mawimbi ya sauti hayafiki kwenye eneo la ‘cochlea’ ili yasafirishwe kwenda kwenye ubongo kupitia mshipa wa fahamu ulioko kichwani matokeo yake mtu hushindwa kusikia vema. “Kuna umuhimu wa kuwa mwangalifu pia katika matumizi ya dawa hata zile za kutibu kifua kikuu (TB) na homa ya mgongo ingawa wapo wengine ambao hupata tatizo hasa wale wanaokuwa wamezaliwa na manjano,” anasema. Ukiziwi husababisha ububu “Hili ni jambo ambalo wazazi wengi hawajui, kwamba mtoto anaposhindwa kuongea katika umri ambao wataalamu tunatarajia awe ameanza kutamka baadhi ya maneno kama baba, mama, kaka au dada, huwa si dalili nzuri. “Wengi wanajipa moyo ni hali ya kawaida hivyo ataongea kadiri anavyokuwa lakini wanashtuka amefika miaka mitatu hajui kuzungumza, matokeo yake wanamtafuta shule za viziwi. Ukweli ni kwamba kwa asilimia kubwa tatizo la usikivu husababisha tatizo lingine la ububu,” anasema. Dk. Liyombo anasema jinsi Mungu alivyouumba ubongo wa mwanadamu kipindi cha umri wa mwaka mmoja hadi miaka sita ndicho anachopaswa kuwa tayari ameweza kujifunza kuzungumza. “Ndiyo maana mtoto huweza kujifunza kwa urahisi lugha yoyote katika kipindi hicho, zaidi ya hapo atajifunza lakini huwa kazi. Ubongo ulivyoumbwa zile seli za usikivu zisipofanya kazi yake sawasawa katika kipindi hicho, huwa pia zinakufa kabisa. “Iwapo imetokea seli hizo zikafa mtoto kushindwa pia kuzungumza lugha yoyote kwani sikio lake hushindwa kupokea mawimbi ya sauti kuyasafirisha kwenye ubongo ili aweze kuwasiliana,” anasema. Gharama za upasuaji Anasema ili kufanikisha upasuaji wa mtoto mmoja iliilazimu serikali kutoa zaidi ya Sh milioni 100 za matibabu nchini India. “Unaweza kuona kwa hawa watoto 45 ilitumia fedha nyingi kiasi gani hadi kufanikisha upasuaji huwa wanakwenda kama awamu nne, kwanza hufanyiwa uchunguzi wa awali ‘mapping’ ambao hugharimu takribani Sh milioni 20,” anasema. Muhimbili kupandikiza kifaa hicho Anasema kutokana na ukubwa huo wa gharama walijikuta wakishindwa kuwahudumia wagonjwa wengi waliohitaji kuwekewa kifaa hicho. “Ndiyo maana miaka mitatu iliyopita tuliandika andiko kwa serikali kuomba Muhimbili tuanze kufanya upasuaji huu nchini, leo hii tumefanikisha na tutafanya kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la Medel,” anasema. Jinsi kinavyofanya kazi Daktari huyo anasema mtoto husika hufanyiwa upasuaji sehemu ndogo ya kichwani ambapo kifaa hicho huwekwa chini ya ngozi na kuunganishwa katika mfumo wa ubongo. “Kisha hupewa kifaa kingine kiitwacho ‘prosser’ ambacho hukivaa katika sikio la nje, hii ‘prosser’ hufanya kazi ya kupokea mawimbi ya sauti na kuyapeleka kwenye kifaa tulichokiweka chini ya ngozi ambapo mawimbi hayo husafirishwa kwenda kwenye ubongo na hivyo mtoto huweza kusikia kama mtu mwingine asiye na tatizo,” anasema. Changamoto Katibu wa Chama cha Wazazi wenye Watoto walio na tatizo la usikivu, anasema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni watoto wao kuporwa mashine hiyo na vibaka wakidhani ni vile vinavyotumika kwenye simu. “Bahati mbaya ni kwamba wakiiba haiwezekani kuuza popote kwa sababu hii mashine kila mtoto ametengenezewa ya kwake, huwezi kuchukua cha mmoja ukampa mwingine, hataweza kusikia. “Kwa hiyo wakiiba wanasababisha hasara kubwa, mtoto anakuwa hawezi tena kusikia na hivi vinanunuliwa kwa gharama kubwa, na lazima uagize kwa kampuni iliyotengeneza, hivyo tunaomba jamii ielewe na itusaidie kwa suala hili,” anasema. Ni upasuaji wa kihistoria Mkurugenzi wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru, anasema kuanza kufanyika kwa upasuaji huo nchini inaifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza kutoa huduma hiyo ya kipekee katika nchi zilizopo kwenye Ukanda wa Jangwa la Sahara.
3
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Emmanuel Amunike amewatema katika kikosi chake hicho kinachojiandaa na fainali za mataifa ya Afrika, wachezaji saba wakiwemo Jonas Mkude na Ibrahim Ajib. Kikosi cha Stars kiliondoka nchini jana kikiwa na wachezaji 32, kwenda Misri ambako kitashiriki fainali za Afcon zitakazoanza kutimua vumbi  kuanzia Juni 21 hadi 19 mwaka huu nchini humo. Wachezaji wengine waliotemwa katika katika hicho ni Kenned Juma, Ayoub Lyanga, Ally Khamis, Ally Ally na Shomary Kapombe ambaye ni majeruhi. Akizungumza jana baada ya kumalizika kwa mazoezi ya mwisho yaliyofanyika katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Amunike alisema anafahamu wanaenda kucheza michuano mikubwa lakini wanaamini watafanya vizuri na kuleta matokeo yenye utofauti . “Tulianza mazoezi Jumapili, nimeweza kuwaangalia wachezaji wote ambao waliweza kujituma na kuonyesha kiwango kizuri kwenye mazoezi ikiwemo pia na nidhamu. “Sijachagua mchezaji kwa kuangalia ukubwa wa jina au kwa sababu anapendwa na mashabiki , nimeangalia ana mchango gani kwenye timu na ataisaidia vipi kwani tunakabiliwa na michuano mikubwa. “Tunatakiwa kuangalia kwa ukubwa, hii ni timu ya Taifa  na bila nidhamu huwezi ukafanikiwa kwenye mpira hivyo anaamini kikosi nilichokichagua kitaleta matokeo yenye utofauti na kufanya vema,”alisema Amunike. Amunike alisema, anafahamu mchezo wa kwanza wataanza dhidi ya Senegal, timu  inayoundwa na wachezaji wakubwa akiwemo Sadio Mane anayekipiga katika klabu ya Liverpool ya England, lakini hilo haliwatishi kwakua wao pia wamejiandaa kiasi cha kutosha. “Hata sisi tuna wachezaji wazuri kama Mbwana Samatta, Simon Msuva, Faridi Mussa na wengine ambao hawana majina makubwa lakini wana uwezo mkubwa, matokeo yataonekana uwanjani. “Nafahamu michuano hii ina presha kubwa lakini tutatumia  kambi yetu ya wiki mbili kujiweka fiti, tutacheza mechi mbili za kirafiki ikiwemo dhidi ya Misri pamoja na Zimbabwe,”alisema kocha huyo ambaye ni  staa wa zamani wa Bareleno na timu ya Taifa ya Nigeria(Super Eagle). Taifa Stars ilifanikiwa kufuzu michuano hiyo, baada ya kuifunga Uganda mabao 3-0, katika mchezo mwisho wa michezo ya kufuzu uliochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Katika fainali hizo, Taifa Stars imepangwa kundi C, pamoja na Algeria, Senegal na majirani zao Kenya (Harambee Stars). Itafungua dimba dhidi ya Senegal maarufu kama Simba wa Teranga Juni 23, kabla ya kuivaa Kenya katika mchezo utakaofuata. Hiyo itakuwa mara ya pili kwa Stars kuchiriki Afcon, mara ya kwanza ilikuwa katika fainali zilizofanyika mwaka 1980 nchini Nigeria
3
NA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM MMILIKI wa klabu ya TP Mazembe, Moise Katumbi, ameipa siri ya ushindi timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, itakayosaidia kuwaua vinara wa soka barani Afrika, Algeria, ili kukata tiketi ya kusonga mbele kwenye michuano ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi. Jumamosi iliyopita TP Mazembe ilikutana na timu ya USM Alger ya Algeria katika mchezo wa awali wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kuichapa mabao 2-1 ugenini na kujitengenezea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa watakaporudiana. Habari za uhakika ambazo zimelifikia MTANZANIA jana kutoka kwa mmoja wa viongozi wa Kamati ya Ushindi ya Stars, zimedai kuwa kigogo huyo alishauri timu hiyo kutumia mbinu walizotumia za kukwepa hujuma ambazo ziliwapa ushindi ugenini dhidi ya wapinzania wao. Amewataka viongozi wa Stars kuhakikisha hawaendi moja kwa moja nchini Algeria kwenye mchezo wa marudiano, badala yake watafute kituo cha karibu ambacho watafikia ili wapate urahisi wa kuunganisha na kutua kwenye ardhi yao muda mfupi kabla ya mechi. “Wenzetu wanadai walilazimika kuweka kituo katika mji wa Marrakech, nchini Morocco, ambapo ni umbali wa kilomita 1,765 kufika Algeria ambapo unaweza kutumia muda wa saa moja kufika nchini humo kwa usafiri wa ndege kutokana na ukaribu uliopo,” alisema kiongozi huyo. Alisema wameshauriwa kutumia njia hiyo kama mbinu ya kusaka ushindi, ambayo itawasaidia kuepuka vitendo visivyo vya kiungwana wanavyoweza kufanyiwa wakiwa nchini humo, ambapo amedai kuwa wameupokea ushauri huo na wataufanyia kazi.
4
KOCHA Mkuu wa Simba, Patric Aussems amedai kutoridhishwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Mtibwa Sugar, ambapo Simba walishinda kwa mabao 2-1.Simba ilitwaa taji hilo ikiwa ni mara yake ya nne, wakati wapinzani wao Yanga wakilitwaa mara tano tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo mwaka 2001.Akizungumza baada ya mchezo huo, kocha huyo amesema dakika 25 za kipindi cha kwanza timu yake haikucheza mpira mzuri na kutoridhishwa na mbinu ya mipira mirefu ambayo ilitumiwa na wachezaji wake na kuahidi kulifanyia kazi suala hilo.“Tumeonesha uwezo mzuri,lakini sikufurahishwa na kiwango cha wachezaji kukaa na mipira, walikuwa wakitumia mipira mirefu na natakiwa kulifanyia kazi kwa mchezo ujao, mimi nina aina yangu ya uchezaji, sitaki kutumia mipira mirefu kwa sababu wachezaji wangu hawana uwezo wa kuitumia,” amesema Aussems.Amesema timu yake ina wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu na katika hilo alisema anataka kumiliki mpira kwa viungo wake kupiga pasi za mwisho zenye uhakika na sio mipira mirefu.Katika mchezo huo, Kiungo Hassan Dilunga na Emanuel Okwi waliumia na kutolewa nje, ambapo kuelekea mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Tanzania Prisons, Kocha huyo alisema atapokea ripoti ya madaktari kujua hali zao kiafya.
4
Rais Kikwete alisema kuwa kiwango hicho kinaufanya uwekezaji wa China katika Tanzania kushika nafasi ya tano kwa thamani ya fedha, na kuwa uwekezaji huo utaiwezesha Tanzania kupata ajira 77,335 baada ya kukamilika kwa miradi yote kukamilika ambayo ujenzi wake unaendelea.Aidha, Rais Kikwete alisema uzuri wa uwekezaji huo kutoka China ni kwamba miradi mingi, 354 kati ya miradi hiyo yote 522 ya wafanyabiashara kutoka China ni kwenye sekta ya uzalishaji.Rais alisema hayo juzi wakati alipofungua Mkutano wa Tatu wa Uwekezaji wa Tanzania na China, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Nyumba ya Kulala Wageni ya Serikali ya Diaoyutai mjini Beijing, China ambako Rais anafanya ziara ya Kiserikali.Akizungumza na wafanyabiashara, Rais Kikwete alisema uhusiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China umekua kiasi cha kwamba kati ya Julai na Septemba mwaka huu, 2014, thamani ya miradi imefikia dola za Marekani milioni 533.9 kulinganisha na miradi yenye thamani ya dola za Marekani 124.14 kwa kipindi cha Julai hadi Septemba mwaka jana.Rais Kikwete alisema ongezeko hilo lilifuatia kufanyika kwa Mkutano wa Pili wa Uwekezaji Kati ya Tanzania na China uliofanyika Dar es Salaam Juni 23 hadi 25, mwaka huu, wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa China katika Tanzania, Li Yuanchao ambaye alifuatana na wafanyabiashara 100.Rais Kikwete alisema pia kuwa biashara kati ya Tanzania na China imeongezeka, lakini kwa kutilia maanani ukubwa wa uchumi wa China ambao ni wa pili duniani kwa ukubwa, bado biashara hiyo inaweza kukua zaidi.
5
Hakuna mwanamke asiyependa kuwa na umbo la kupendeza na umbo bila tako si umbo. Wengi wanawake hufanya kila nia kuhakikisha kuwa wanapata umbo wanalotaka, wengine wakienda kiasi cha kufanyiwa upasuaji na wengine kutumia matembe almuradi wawe na makali mazito. Si hayo tu wapo baadhi ambao huvalia nguo kadhaa ama kutumia makalia bandia ili kuonekana warembo. Hizi hapa njia rahisi za kunenepesha makalio bila kupata taabu yoyote. Kuinama Simama imara na uhakikishe kuwa mgongo wako umelainika kisha uiname sawa na mtu anayetaka kukaa hakikisha kuwa magoti yako hayapiti viganja vya miguu. Rudia hii mara 3 hadi unapokamilisha raundi 20. Kuruka na kuinama Panua miguu huku umesimama kisha uiname na kutia mikono miwili kati kakati ya miguu chini. Rudia hii mara kadhaa huku ukiruka na kurudi katika nafasi hiyo hiyo. Hakikisha kuwa unanyoosha magoti ukiendelea kuridia zoezi hili. Kuinukia kwa mgongo Lala kichalichali  kisha uikunje miguu na mikono yako iuweke kando kando. Kaza mikono kisha uinuke kwa mgongo na uhakikishe kuwa mgongo huo unasalia kuwa laini. Rudia hii pole pole mara sita. Mazoezi haya unatakiwa kufanya mara tatu kwa wiki ili kupata matokeo ya haraka. Hakikisha kuwa unakunywa maji ya kutosha na kupunguza vyakula vyenye mafuta.
4
CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Shule kuu ya Sheria imeanzisha kituo cha msaada wa kisheria kitakachotoa huduma ya kisheria bure kwa wakazi wenye changamoto za kipato.Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Utafiti na Majarida, Ubunifu, Ushauri na Ushirikiano wa UDOM, Profesa Flora Fabian wakati akifungua mafunzo ya wafanyakazi wa Ustawi wa Jamii mwishoni mwa wiki.Akizungumzia warsha hiyo iliyofanyika chini ya miradi ya Elimu ya Haki za Ulemavu na Kituo cha Msaada wa Kisheria (DRELAC) na kuwashirikisha wafanyakazi 30 wa Ustawi wa Jamii kutoka Mkoa wa Dodoma, alisema imelenga kuwajengea uwezo kujua haki za ulemavu, sheria na sera ya kitaifa kwa watu wenye ulemavu.Profesa Fabian alisema Shule Kuu ya Sheria ya UDOM imekuja na wazo la kuanzisha Kituo cha Msaada wa Kisheria baada ya kubaini kuwapo kwa watu wengi ambao wamekuwa wakitafuta msaada wa kisheria ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kusisitiza kuwa kituo hicho kitafanya kazi kwa kushirikiana na ofisi hiyo.Naye, Kaimu Amidi wa Shule Kuu ya Sheria ya Chuo Kikuu cha UDOM, Victorino Kuluchumila alibainisha kuwa kituo hicho cha Msaada wa Kisheria itaiwezesha taasisi hiyo kutekeleza moja ya malengo yake makuu ya kutoa huduma kwa jamii.
3
NA MWANDISHI WETU – DAR ES SALAAM SIKU chache baada ya Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe kutangaza kujiuzulu kwa shinikizo la jeshi la nchi hiyo, ambalo lilidai kuwa amezungukwa na wahalifu, gumzo limetanda kuhusu hatma ya viongozi wengine katika nchi kadhaa barani Afrika ambao wametawala muda mrefu zaidi. Mugabe alitangaza kujiuzulu mapema wiki hii katika kipindi ambacho Spika Jacob Mudenda alikuwa akijiandaa kuliongoza Bunge kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye, msingi ukiwa ni baada ya Jeshi kuonekana kupenyeza ajenda yake hadi ndani ya chama chake cha ZANU-PF. Kiongozi huyo hakujiuzulu urais pekee, bali pia alifutwa madaraka ya kiongozi mkuu wa chama chake cha ZANU-PF na mkewe Grace kuvuliwa uanachama na kuondolewa katika nafasi ya mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama hicho. Wakati jeshi likifanikiwa kupenyeza ushawishi wake na kuhitimisha utawala wa miaka 37 ya Mugabe, swali kubwa na ambalo limezua mjadala katika baadhi ya vyombo vya habari vikubwa duniani, mitandao ya kijamii na katika nchi ambazo zimeishi tawala za aina hiyo, ni kuhusu hatma ya viongozi takribani 12 barani Afrika, ambao wapo madarakani kwa muda mrefu. Viongozi hao ni pamoja na Rais wa Guinea ya Ikweta, Teodoro Obiang Nguema,  Omar al Bashir (Sudan),  Idriss Deby (Chad), Issayas Afewerki (Eritrea), Paul Biya (Cameroon) na Yoweri Museveni (Uganda). Wengine ni Rais wa Congo Brazaville Denis Sassou Nguesso, Abdelaziz Bouteflika (Algeria), Paul Kagame (Rwanda), Joseph Kabila (DR Congo), Faure Gnassingbe  (Togo) na Pierre Nkurunziza (Burundi). Wakati Mugabe akiwa ameondoka na kuacha taswira ya kiongozi aliyekuwa akiongoza kwa kukaa madarakani muda mrefu zaidi, pengine  hilo likichochewa zaidi na mgogoro wake na nchi za Magharibi, lakini ukweli ni kwamba alikuwa akishika nafasi ya pili nyuma ya Rais Nguema wa Guinea ya Ikweta. Nguema ndiye anayeshika nafasi ya kwanza barani Afrika kwa kutawala nchi hiyo kwa miaka 38, akiingia madarakani  mwaka 1979. Tofauti yao ni kwamba wakati Mugabe akishika rekodi ya kuwa kiongozi mkongwe zaidi duniani akiwa na miaka 93, Nguema yeye licha ya kutawala muda mrefu zaidi, ana umri wa miaka 75 kama ilivyo kwa mrithi wa Mugabe, Emmerson Mnangagwa. Watu wanaofuatilia siasa za Afrika watakuwa wanakumbuka jinsi ambavyo Nguema aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi yaliyofanyika Agosti 3, 1979 yakimtoa kwenye utawala mjomba wake, Francisco Macias Nguema, ambaye alipigwa risasi na kikosi cha rais huyo. Wakati mijadala mikubwa iliyotawala katika taarifa za vyombo vya habari ikishauri viongozi hao kusoma alama za nyakati kama alivyofanya Jose Eduardo Dos Santos wa Angola ambaye mwaka huu aling’atuka kwa hiari baada ya kutawala kwa miaka 38, Cameroon nayo imenyooshewa kidole. Rais Biya ambaye hadi sasa ametawala miaka 35 tangu aingie madarakani mwaka 1982 na kabla ya hapo Waziri Mkuu kwa kipindi cha miaka saba, tayari wapinzani wake wamesema walikuwa wakifuatilia kwa ukaribu matukio ya Zimbabwe. Franck Essi, ambaye ni Katibu Mkuu wa chama cha upinzani cha Cameroon Peoples, mapema wiki hii alikaririwa na Shirika la Habari la Reuters akisema viongozi wanatakiwa kusoma alama za nyakati. “Viongozi lazima waweke kwenye mstari mabadiliko ya kidemokrasia na ya uongozi wa mpito kwa njia ya amani, ambayo itawezesha uongozi mpya. Ikiwa si sasa au baadae, watu walioishiwa pumzi wataamka,” alisema. Mbali na Biya, Rais wa Uganda, Museveni  ambaye hadi sasa ametawala nchi hiyo kwa miaka 31 tangu alipoingia madarakani Januari mwaka 1986 baada ya kumpindua Idd Amin Dada kwa msaada mkubwa wa Serikali ya Tanzania, naye huenda ametikiswa na tukio la Zimbabwe. Museveni ambaye Februari mwaka 2016 alichaguliwa kuongoza muhula wa tano licha ya kutuhumiwa kufanya udanganyifu katika uchaguzi ili kujipatia ushindi, saa chache baada ya Mugabe kulazimishwa kuondoka madarakani, Reuters iliripoti kuwa aliandika katika akaunti yake ya tweeter akisema kuwa ameongeza mishahara kwa watumishi wa umma, sambamba na kuliimarisha jeshi. “Sasa uchumi Uganda umeimarika, Serikali imeweza kuangalia uwezekano wa kuongeza mishahara kwa wanajeshi, watumishi wa umma, afya na walimu na kushughulikia suala la makazi,” aliandika Museveni jambo ambalo Reuters katika uchambuzi wake, imesema alifanya hivyo kwa kuogopa kivuli cha Zimbabwe. Reuters ilikwenda mbali na kuponda kauli yake na kuhoji uchumi ambao alisema unakua wakati ukuaji wake ni mdogo mno, huku idadi ya watu milioni 37, wengi wao matumizi yao kwa siku ni chini ya dola moja. Waliojadili mjadala huu, wamekumbusha jinsi ambavyo nyakati zilivyobadilika hasa ikizingatiwa kuwa mwaka huu si tu haukuwa mzuri kwa Mugabe, bali hata kabla ya hapo kwa Yahya Jammeh wa Gambia ambaye utawala wake wa miaka 22 ulihitimishwa na matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi mpinzani wake, Adama Barrow wa chama cha United Democratic Party (UDP). Kwa sababu kama hizo, ukimwacha Museveni, mwingine anayeangaliwa kwa jicho tofauti la uchambuzi wa utawala bora kutokana na kukaa madarakani muda mrefu ni Nguesso wa Congo Brazaville, ambaye ametawala kwa miaka 33 sasa. Nguesso alitwaa madaraka kwa mara ya kwanza mwaka 1979 hadi 1992, na kurudi baadaye mwaka 1997 katika kipindi cha mwisho cha vita ya wenyewe kwa wenyewe. Machi 2016 alichaguliwa tena kuongoza nchi hiyo  na wachambuzi wa mambo wanasema kuna uwezekano akagombea kwa mara nyingine baada ya kipindi cha sasa kumalizika. Mjadala wa sasa haujamwacha Rais al Bashir wa Sudan, ambaye naye anatajwa kuliongoza taifa  hilo kwa mwaka wa 28 sasa tangu alipoingia madarakani Juni 1989. Al Bashir aliingia madarakani alipokuwa Brigedia wa Jeshi na kuongoza kikosi kilichompindua waziri mkuu wake, Sadiq al-Mahdi. Anayemkaribia Al Bashir ni Rais wa Chad, Deby, ambaye alichukua madaraka Desemba 1990  na hivyo kufanya miaka aliyokaa madarakani kufikia 27 hadi sasa. Katika orodha hiyo, wamo pia Afewerki wa Eritrea, ambaye amekaa madarakani kwa miaka 24 sasa pasipo kuonyesha dalili za kuachia ngazi. Wengine ni Bouteflika ambaye ametawala Algeria kwa miaka 18 sasa, sawa na Ismail Omar Guelleh wa Djibouti. Kagame,  ambaye ametawala Rwanda kwa miaka 17 hadi sasa ingawa amekwishatangaza kuwa anaondoka kipindi cha mwisho hadi mwaka 2024, lakini wachambuzi wanasema lolote linaweza kutokea, kwamba itategemea na upepo utakavyokuwa. Rais Kabila naye anaingia katika orodha hiyo akiwa ametawala DR Congo kwa kipindi cha miaka 16 na kuna kila dalili za upepo wa Zimbabwe kuivuruga Serikali yake. Baada ya vuguvugu la kumwondoa Mugabe kuanza, Jean-Pierre Kambila, ambaye ni msaidizi wa  Kabila, aliandika katika ukurasa wake wa tweeter  kuwa maandamano ya Zimbabwe yaligubikwa na ukoloni. “Maandamano yaliyotengenezwa yalichochewa na wale wote ambao hawakubali uhuru wa Afrika. Akina Mugabe wengine watazaliwa. Hakuna kitu cha kuhangaika,” aliandika. Itakumbukwa Kabila aliahirisha uchaguzi kwa mara nyingine baada ya kukataa kuachia madaraka jambo ambalo lilizusha maandamano. Mbali na Kabila, Rais Gnassingbe naye anaingia katika orodha hii akitajwa kuongozwa na kiburi ambacho kimemfanya agome kuondoka madarakani ambako amekaa kwa miaka 12 awali akiwa waziri katika uongozi wa baba yake, ambaye baada ya kufariki akarithishwa nafasi hiyo akisaidwa na Jeshi. Kama Gnassingbe, Rais Nkurunziza naye amedumu madarakani kwa miaka 12 hadi sasa ingawa mwaka  2015 alinusurika katika jaribio la mapinduzi ya kijeshi baada ya kushuhudiwa utata mkubwa katika uteuzi wake kugombea urais kwa muhula wa tatu. Baadhi ya wachambuzi wanasema pamoja na kwamba anguko la Mugabe limeleta mtikisiko barani Afrika, hasa ikizingatiwa kuwa upande wa kaskazini ulikwishashuhudia vuguvugu katika nchi za kiarabu ‘Arab Spring’, licha viongozi wengi wapya kuonekana kupwaya ukilinganisha na wale wa zamani,  bado hakutawafanya wananchi warudi nyuma kudai uongozi unaoheshimu katiba na kuacha kuzifinyanga kwa masilahi binafsi. WALIOACHA REKODI KUBWA Ukimwacha Mugabe, viongozi wengine ambao hawako madarakani sasa, lakini wameacha rekodi ya kutawala muda mrefu ni pamoja na Mfalme Haile Selassie ambaye ameongoza Ethiopia kwa miaka 44 kabla ya kutimuliwa madarakani mwaka 1974. Mwingine ni Rais wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi ambaye alitawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 42 kabla ya kung’olewa mwaka 2011 kwa ushirikiano kati ya majeshi ya Kujihami ya Umoja wa Nchi za Magharibi (NATO) na kikosi cha waasi kutoka Benghazi. Rais wa zamani wa Gabon, Omar Bongo Ondimba aliongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 41 kabla ya kufariki dunia Juni mwaka 2009.
2
Raymond Minja -Iringa MEYA wa Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe (Chadema), amekalia kuti kavu linalohatarisha nafasi yake kabla ya muda wake kumalizika miezi mitatu ijayo. Zikiwa zimesalia siku 90, madiwani wa halmashauri hiyo wamemtuhumu kwa makosa kadha katika makundi manne ambayo yanaweza kusababisha apigiwe kura ya kutokuwa na imani naye. Barua ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Ahamed Njovu iliyoandikwa kwenda kwa meya huyo na kusambazwa kwa vyombo vya habari jana, imetaja makosa kuwa ni pamoja na matumizi mabaya ya ofisi. Pia anatuhumiwa kufanya matumizi bila kuzingatia kanuni za kudumu za halmashauri, kinyume na taratibu na aliamuru baadhi ya wajumbe wa halmashauri kufanya ziara mikoa ya Njombe na Mbeya pasipo mkuu wa mkoa kujiridhisha kinyume na kanuni za kudumu za halmashauri. Aidha anahusishwa na kugawa nafasi za kamati kwa upendeleo kwa kigezo cha tofauti za kisiasa na chuki binafsi na anadaiwa kumiliki mali zisizoendana na kipato chake Pia anadaiwa kujipatia tenda za kufanya kazi za halmashauri kwa kutumia majina ya rafiki zake wa karibu wenye kampuni za kandarasi. Kosa la pili, ni matumizi mabaya ya rasilimali za halmashauri, ikiwa ni pamoja na kutumia gari kwa kazi binafsi kinyume na kanuni za halmashauri. Katika kosa la tatu, anatuhumiwa kuwa na mwenendo mbaya na ukosefu wa nidhamu.  Kosa la nne, anatuhumiwa kushiriki vitendo vya rushwa katika ofisi yake jambo ambalo haliendani na kanuni za halmashauri. Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, amekiri kupokea maombi yaliyosainiwa na wajumbe 19 wa halmashauri yakitaka kufanyika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani kujadili kumwondoa madarakani. Kanuni za kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Iringa za mwaka 2015, kifungu namba 5, kifungu kidogo cha 2 hadi 7, kinaagiza baada ya mtuhumiwa kupokea maombi ya tuhuma zinazomkabili, anatakiwa kuwasilisha majibu yake ndani ya siku tano. Baada ya kupokea utetezi, mkurugenzi alisema atamwarifu mkuu wa mkoa tuhuma zinazomkabili meya pamoja na utetezi wake ili kuzipitia. “Baada ya mkuu wa mkoa kupokea taarifa, ataunda timu ya uchunguzi ya kushughulikia tuhuma hizo na timu hiyo baada ya kukamilisha kazi yake na kuwasilisha taarifa yake, mkuu wa mkoa atawasilisha taarifa kwa mkurugenzi wa manispaa,” alisema. Alisema baada ya kupokea taarifa hiyo, ndani ya siku 14, mkurugenzi atawasilisha kwenye Baraza la Madiwani kwa uamuzi wa tuhuma zinazomkabili muhusika. Alipoulizwa kuhusu sakata hilo, Kimbe alikiri kupokea barua yenye tuhuma hizo na akaahidi kutoa ufafanuzi wake katika kikao alichotarajia kufanya na waandishi wa habari jana jioni.
3
KOCHA wa Lipuli FC, Suleiman Matola amesema kucheza kwa kujituma na kutanguliza malengo ni mbinu itakayokisaidia kikosi cha Simba kuibuka na ushindi kwenye mchezo wao kimataifa dhidi ya Nkana FC ya Zambia na kutinga hatua ya makundi.Mchezo huo wa raundi ya pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika, unatarajiwa kupigwa kesho kwenye uwanja wa taifa wa Dar es Salaam, baada ya ule wa awali uliopigwa Kitwe, Zambia wenyeji Nkana kupata ushindi wa mabao 2-1.Akizungumza na gazeti hili jana Matola, alisema bingwa huyo mtetezi wa Ligi Kuu ana kikosi kizuri na kipana na kwamba kinachotakiwa kwa wachezaji wake ni kufuata maelekezo ya kocha wao na kucheza kwa nidhamu ili kupata ushindi. “Wachezaji wa Simba wanatakiwa kujiandaa vizuri, wasibweteke na bao walilolipata ugenini, Nkana ni timu nzuri,hata wachezaji wa Simba ni wazuri pia kinachotakiwa kocha wa Simba Patrick Aussems kuhakikisha anatengeneza muunganiko mzuri wanaweza wakapata mabao mengi,”alisema Matola aliyewahi kuwa mchezaji wa kikosi hicho na hatimaye kocha msaidizi.Alisema wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanawazuia washambulia wa wapinzani wao wasipate nafasi ya kufunga bao na kuhakikisha wanatumia vyema nafasi watakazozipata ili kuhakikisha katika kipindi cha kwanza wanapata bao la mapema ili kuwachanganya wapinzani hao kama walivyofanya kwa Mbabane Swallows, eSwatini walioshinda jumla ya mabao 8-1.Katika mchezo huo wa kesho timu itakayoibuka na ushindi katika itafuzu hatua ya makundi. Ushindi wa bao 1-0 utaivusha Simba na kurudia historia ya mwaka 2003 ilipotinha hatua ya makundi kwa kuifunga Zamalek ya Misri. Nahodha wa timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 17, ‘Serengeti Boys’ Abraham Morice (kulia) akichezesha droo ya fainali za AFCON U-17 katika hafla iliyofanyika juzi Mlimani City, Dar es Salaam.Kushoto ni mchezaji wa zamani wa Taifa Stars, Adolf Rishard. (Picha na Rahel Pallangyo) JUVENTUS, Italia CRISTIANO Ronaldo anatarajiwa kucheza dhidi ya Roma leo kabla ya kupumzishwa katika moja ya mechi mbili za ‘fainali’ kwa mwaka 2018, Massimiliano Allegri alithibitisha. Bosi huyo wa Juve aliahidi nkumpa nyota huyo wa Ureno angalau mechi moja Desemba huku Ronaldo akicheza dakika 90 kwenye mechi zote za Serie A isipokuwa moja msimu huu.Allegri anataka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 kucheza dhidi ya Roma, wakati Juve ikiwania kuendeleza rekodi yake ya kutokufungwa katika kutetea taji lao, lakini anafuraha kuona Ronaldo akikosa safari ya kwenda Atalanta kwenye ‘Boxing Day’ au kwenye mechi dhidi ya Sampdoria Desemba 29. “Ronaldo atacheza kesho (leo), kisha atakosekana katika mechi mbili zijazo,” alisema Allegri kwneye mkutano na waandishi wa habari jana.Mechi ya leo katika uwanja wa Allianz Juve inakutana na Roma iliyocheza mechi tano mfululizo bila ushindi kwenye michuano yote kabla ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Genoa Jumapili iliyopita. Presha iko kubwa kwa kocha mkuu Eusebio Di Francesco, lakini Allegri alisisitiza ushindi. “Ni timu nzuri, pamoja na mambo mengine, ni timu pekee ya Italia pamoja na Juventus bado zipo kwenye Ligi ya Mabingwa,” alisema.
4
NEW YORK, MAREKANI RAIS Donald Trump, jana ameyaonya mataifa kutothubutu kufanya biashara na Iran, huku akisifu vikwazo vipya dhidi ya taifa hilo kuwa vikali zaidi kuwahi kuwekwa, hatua iliyoibua mchanganyiko wa ghadhabu, hofu na uasi nchini humo. Kupitia ukurasa wake wa twitter, Trump aliandika kuwa vikwazo dhidi ya Iran tayari vimeshawekwa. “Hivi ni vikwazo vikali zaidi kuwahi kuwekwa, na Novemba tutangaza vikwazo vingine,” aliongeza Trump. Aliongeza kuwa yeyote anayefanya biashara na Iran, hatafanya biashara na Marekani, na kwamba anachokitafuta ni amani duniani, na si zaidi ya hapo. Muda mfupi tangu kuanza kutekelezwa kwa vikwazo hivyo, kampuni ya magari ya Ujerumani ya Daimler, ilitangaza kusimamisha biashara zake nchini Iran. Taarifa ya Daimler ilisema wamesitisha shughuli nchini humo kutokana na vikwazo hivyo vilivyoanza kutekelezwa, na kuongeza itaendelea kufuatilia kwa karibu hatua za kisiasa. Wairan wengi, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara wa magari, wanailaumu Serikali yao kwa kurejeshwa vikwazo hivyo vya Marekani, lakini pia wanahofia huenda vikawa ni pigo la mwisho kwenye uchumi wa taifa hilo unaoyumba. Kujiondoa kwa Trump kwenye mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015, Mei mwaka huu, tayari kuliwaogopesha wawekezaji na kuchochea kushuka kwa thamani ya sarafu ya Iran – riali, kabla hata ya vikwazo hivyo kuanza kutekelezwa upya. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mohammad Javad Zarif, amewaambia wanahabari kuwa namna ambavyo dunia imeijibu hatua hiyo ya Trump, imeonyesha kutengwa kwa Marekani kidiplomasia. Mmoja wa wafanyakazi wa sekta ya ujenzi, alisema akiwa katika mtaa mmoja mjini Tehran, anajisikia kama maisha yake yamevurugika. Alisema vikwazo hivyo tayari vimekwishaathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya watu, na kwamba hawezi hata kununua chakula, wala kulipa kodi ya nyumba. Serikali za Ulaya zimeeleza kughadhabishwa na mkakati huo wa Trump, unaosababisha biashara zao zilizopo Iran kukabiliwa na kitisho cha kuadhibiwa kisheria na Marekani.
2
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge (pichani) amewaagiza maofi sa mipango miji na wapima ardhi kutumia ujuzi na utaalamu wao kulisaidia taifa, badala ya kusubiri majengo yasimame ndipo wawavunjie watu.Dk Mahenge alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa maofisa mipango miji na wataalamu wa ardhi yaliyoratibiwa na Shirika la African Institution For Capacity Development (AICARD) na kushirikisha wataalamu hao kutoka mikoa ya Singida, Morogoro, Iringa na Dodoma.Katika hotuba ya Dk Mahenge iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri, alisema wataalamu hao wanatakiwa kufanya kazi kwa umakini mkubwa kwa kuwa miji mingi inakuwa kwa kasi kutokana na ongezeko la watu. Aliwataka kuongeza kasi ya kupanga miji katika maeneo yote na isiwe mijini pekee kwani hata vijijini kuna ongezeko kubwa la ujenzi wa majengo kutokana na miundombinu kuboreshwa ikiwemo umeme wa Wakala wa Umeme Vijijini(REA).“Ongezeni kasi ya kupanga miji, watu wamekuza uchumi na wanataka kujenga majengo mazuri, wanashindwa kutokana na kutopangwa kwa miji na hata wakijenga hayana mpangilio mzuri na matokeo yake baadaye wanakuja kuvunjiwa kwa kuambiwa hawajajenga panapostahili,”alisema.Aliyataka mashirika yanayotoa elimu kuwashirikisha wenye mamlaka katika halmashauri wakiwemo wakurugenzi kwani ndiyo wenye maamuzi. Alisema lengo la kufanya hivyo ni kuondoa migongano inayotokea kwenye halmashauri kwa kutoelewana kwa wakurugenzi.Naye Mkurugenzi wa AICARD, Profesa Dominick Byarugaba alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwakumbusha wataalamu hao wajibu wao katika kipaumbele cha upangaji miji kwa kuwa hakuna maendeleo mazuri miji isipopangwa vizuri. Alisema mafunzo hayo ambayo yamepewa jina la ‘Spatial Planning’ni moja ya mikakati ya Shirika la AICAD ya kujenga uwezo wa maofisa mipango katika kupambana na umaskini unaotokana na athari zitokanazo na mipango isiyokuwa sahihi.“Tumewafundisha Kenya tukaenda Uganda na sasa tupo hapa Tanzania ambapo miji inakuwa kwa kasi kubwa ikiwemo Dodoma, tunaomba mkafanye kazi kubwa katika maeneo yenu na kuwaelimisha na wengine ili tufiki uchumi wa kati na kupunguza kasi ya uhamiaji wa watu kutoka vijijini kwenda mijini,”alisema.Kaimu Mkurugenzi wa Mipango kutoka Chuo Kikuu Huria(OUT), Benjamini Mbusu alisema kada ya mipango ndiyo chachu ya maendeleo kwa taifa lolote hasa linalopiga hatua za kimaendeleo kama Tanzania. Mbusu alisema mipango ya kuipanga nchi ikitumiwa vizuri, hakutakuwa na kelele katika maeneo ya miji na miji midogo ambayo ndiyo dira ya maendeleo.
3
MARGRETH MWANGAMBAKU(TUDARCO) Na TUNU NASSOR DAR ES SALAAM WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, William Lukuvi amewaongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Emmanuel Mwambulukutu. Balozi Mwambulukutu alifariki dunia Agosti 13, mwaka huu nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu. Viongozi wengine waliokuwa katika msiba huu ni Mbunge na Mke we Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete , Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba,  Mbunge wa zamani wa Lupa, Njelu Kasaka,  Philip Magani pamoja na Jaji Mstaafu  Damian Lubuva. Akizungumza wakati wa kuaga mwili huo, Waziri Lukuvi alisema marehemu Mwambulukutu atakumbukwa kwa uchapakazi wake kwani ndiye aliyeanzisha ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini. “Nilimpenda kwa kuwa alikuwa mwadilifu na jasiri na hajawahi kuwa na rekodi ya kugombana na mtu yeyote na alikuwa mwanadiplomasia kabla hata ya kuwa balozi,” alisema Lukuvi. Akimzungumzia marehemu, mke wa Rais Mstaafu Salma Kikwete,  alisema Mwambulukutu alikuwa ni mtu mwenye imani na aliyependa familia. “Wakati mzee (Rais Jakaya Kikwete) akiwa waziri yeye alikuwa naibu waziri hivyo tuliishi naye kama familia, nimekuja kumpa pole mke wa marehemu kama dada yangu kwa kufiwa na mumewe,” alisema Mama Salma. Kwa upande wake Njelu Kasaka alisema Mwambulukutu alikuwa anajituma kazini na hakuwahi kuwa na mgogoro na mtu. “Alikuwa mcheshi na mwenye kujituma na hajawahi kuingia katika mgogoro na mtu hadi umauti unamfika,”  alisema Kasaka. Marehemu Mwambulukutu alizaliwa Novemba 22, 1944 Tukuyu Mkoani Mbeya na ameacha mjane na watoto wanne.
3
Morocco Sheria mpya ya kupambana na unyanyasaji wa kingono na udhalilishaji wa mwanamke nchini Morocco, itaanza kutekelezwa hivi karibuni. Sheria hiyo ambayo inafanya suala hilo lionekane ni uhalifu inajumuisha upigaji marufuku wa ndoa za kulazimishwa. Sheria hiyo imefikiwa kutokana na kuongezeka kwa hali ya wasiwasi katika miaka ya hivi karibuni juu ya kiwango cha udhalilishaji wanawake. Kwa mujibu wa sheria hiyo, kwa yeyote atakayetiwa hatiani kwa kosa la kudhalilisha kingono hadharani iwe kwa kutumia maneno au ishara yoyote ya kudhalilisha kijinsia atakabiliwa na hukumu ya kifungo kuanzia mwezi mmoja mpaka sita gerezani na faini ya fedha taslimu. Sheria hiyo mpya imepokelewa vizuri lakini pia imekosolewa kwa sababu haifafanui vizuri juu ya unyanyasaji huo majumbani na vitendo vya ubakaji ndani ya ndoa. Shirika la haki za binadamu inasema kuwa wanawake wengi nchini Morocco, wamekuwa waathirika wa matukio ya unyanyasaji wa kingono. Katika ripoti yake ya mwaka 2015, Shirika la Haki za Binadamu nchini humo imeeleza kuwa zaidi ya asilimia 20 ya wanawake nchini Morocco, wamekumbwa na matukio ya unyanyasaji wa kingono japo mara moja katika maisha yao.  
2
KIUNGO wa klabu ya Juventus, Paul Pogba, ameanza safari yake kutoka jijini Los Angeles nchini Marekani na kuelekea jijini Manchester kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na mashetani wekundu, Manchester United. Mchezaji huyo amekuwa akisubiriwa kwa muda mrefu kuweza kukamilisha usajili huo ambao unadaiwa kuwa utavunja rekodi ya usajili duniani, lakini inadaiwa kwamba muda wowote kuanzia sasa atakuwa anamalizana na klabu hiyo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, anatarajia kumalizana na klabu hiyo kwa kitita cha pauni milioni 100 na kutaka kufunika usajili ambao unaonekana kuwa wa fedha nyingi wa Gareth Bale wa kujiunga na klabu ya Real Madrid akitokea klabu ya Tottenham kwa kitita cha pauni milioni 86. Uhamisho wa Bale ni usajili wa pekee ambao umetikisa duniani na kudaiwa kuwa ni kiasi kikubwa cha fedha ambacho kimetumika, lakini huu wa Pogba unataka kuvunja rekodi za usajili duniani. Kupitia akaunti yake ya Twitter, Pogba ameweka picha yake ambayo inamuonesha akitokea jijini Los Angeles na kuelekea jijini Manchester na kuandika kwamba ‘Mungu ni mkubwa’. Hii ni ishara tosha ya kuwaonesha mashabiki wa Manchester United kuwa tayari amekubaliana na uongozi wa klabu hiyo, kilichobaki ni kuuweka wazi usajili wake. Hata hivyo, mchezaji huyo aliandika kwamba safari yake ilichelewa kutokana na masuala hayo ya michezo, lakini kwa sasa kila kitu kipo sawa.
4
    Na JANETH MUSHI-ARUSHA MEYA wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro (Chadema), amesema Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, amewataka wazazi na walezi wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Lucky Vincent waliofariki dunia kwa ajali, wakubali sehemu ya rambirambi zao zikarabati Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru. Kauli hiyo aliitoa mjini hapa jana katika ofisi za Chadema Kanda ya Kaskazini alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kuachiwa kwa dhamana yeye na viongozi wengine 12, wakiwamo wa Shirikisho la Wenye Shule na Vyuo Binafsi Tanzania (Tamongsco) walioshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa siku mbili baada ya kukamatwa walipokwenda kutoa rambirambi kwa wazazi na walezi hao. Wengine waliokamatwa ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Ephraim Jackson, Diwani wa Olasiti, Alex Martin, Katibu wa Mbunge wa Arusha Mjini, Innocent Kisanyaga, Katibu wa wa Tamongsco Kanda ya Kaskazini, Leonard Mao na viongozi wengine wa dini. Lazaro alidai kuwa Gambo aliwaita wazazi na walezi hao wiki iliyopita katika Hoteli ya Mount Meru kwa chakula cha mchana na kuwaeleza kuwa kiasi cha Sh milioni 56 zilizotolewa na wadau mbalimbali kwa familia hizo zitumike kukarabati hospitali hiyo. “Cha kunisikitisha zaidi ameita wafiwa Mount Meru Hotel, amewapeleka ‘lunch’, ananikamata mimi kukutana na wafiwa kwenye shule ya wanafunzi waliopata ajali kwa ajili ya kuwapa mkono wa pole, yeye amewaita Mount Meru Hotel, amewasumbua wafiwa kutoka kwenye kata zetu, kwanini yeye asikamatwe? “Halafu anawaambia eti fedha zilizobaki, shilingi milioni 56, zikakarabati Hospitali ya Mount Meru, ni lini rambirambi zinaenda kutekeleza Ilani ya CCM? Nataka nihoji Rais Dk. John Magufuli, mimi ni Meya wa Jiji, natekeleza shughuli za jamii hapa, Serikali imesema inaleta fedha kwenye miradi, ni kwa nini Mkuu wa Mkoa anashinikiza fedha za rambirambi zilizobaki zikakarabati hospitali?  “Eti fedha hizo zikatekeleze ilani ya CCM, ilani ya CCM inatekelezwa kwa fedha za rambirambi? Haya tusipofiwa, kusipokuwa na maafa hiyo ilani itatekelezwaje? Hiyo hospitali tutakarabati kwa namna gani kama hakutatokea maafa?” alihoji. Pia alidai kuwa Gambo amepeleka kiasi kingine kwa familia ya watu walioangukiwa na mti hivi karibuni huku fedha hizo zikiwa hazijatolewa kwa shughuli hiyo. Alidai kuwa Gambo amepeleka Sh milioni 1.5 katika Kata ya Sambasha kwa familia tatu ambazo maharusi wake walifariki Februari, mwaka huu baada ya kusombwa na mafuriko yaliyotokana na mvua zilizokuwa zikiendelea kunyesha na kuhoji rambirambi hiyo isingekuwapo angepeleka fedha kutoka wapi. “Hizo fedha alipeleka kwenye familia tatu wakati walifiwa familia tano, hiyo fedha alimpa mkuu wa wilaya na alitangaza, ndiyo maana hizi taasisi wakaona kwa vile mkuu wa mkoa hana utaratibu unaoeleweka ambao uko wazi, wakaona waende moja kwa moja kwa wahusika, namna ya kuwapata wahusika ni sisi viongozi wa maeneo husika. “Kwa hiyo niseme mkuu wa mkoa akitaka kuongoza vizuri, awe na utaratibu unaoeleweka. Huu uongozi wa ubinafsi kwenye mkoa na Jiji la Arusha sisi hatutakubali, wenyeviti wa halmashauri za mkoa huu na ma- DC wetu na wakurugenzi hatutakubaliana na mkuu wa mkoa anayefanya biashara binafsi, shughuli za umma anafanya binafsi, hatuwezi kuwa na ‘one man show leadership or business’,” alisema. Pia alisema kuwa Gambo ameletwa kuongoza mkoa huo, hivyo anapaswa kumshirikisha yeye, wabunge, wenyeviti wa halmashauri, wakuu wa wilaya na wakurugenzi katika shughuli za kijamii.  “Maafa haya yametokea, Gambo anasimamia msiba mwenyewe, wakati tukio lilipotokea hakuwepo ila viongozi wengine wa ngazi za wilaya na mkoa walilishughulikia, haiwezekani anataka fedha za jiji zitumike kwenye gharama za mazishi, lakini kwenye shughuli hiyo hataki viongozi tushiriki. “Hatuwezi kuwa na uongozi wa aina hii na nimweleze tu Magufuli, tuna nia njema na nchi hii, sisi ni viongozi tuliochaguliwa na wananchi, lakini ajue kwamba kuna tatizo, kiongozi wake aliyemleta kwenye mkoa huu ni mbinafsi na mimi siwezi kufanya kazi na kiongozi ambaye ni mbinafsi, kazi za wananchi zinatakiwa zifanyike kwa uwazi,” alisema. Alisema Gambo atakuwa kiongozi wa kuonyesha mfano, uwazi kwenye uongozi wake na jamii kwa ujumla, iwapo kuna mtu au taasisi inataka kutoa rambirambi ataielekeza kwenye familia husika kwa sababu tangu mwanzo hakuwa wazi. Alidai kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqqaro, hajui kinachoendelea katika suala la rambirambi. “Hajui namna zinavyogawanywa, angekuwa kiongozi anayeelewa ushirikishwaji kwa wenzake, jambo hili angeshirikisha wakuu wa mikoa ya Manyara na Kilimanjaro.  “Angesema meya ni mpinzani, mbunge ni mpinzani sawa tungekaa mbali, awashirikishe basi hawa CCM wenzake, Joel Bendera sio Chadema, kwa nini anawatenga wenzake na wamechaguliwa na rais? Huyu ni kiongozi msiri, hili ameshughulika nalo mwenyewe.  “Na nasema atalibeba mwenyewe na nitaendelea kufuatilia fedha zilizopelekwa kwa wafiwa ili wapate kwa usahihi bila udanganyifu na kwenye hili najua Magufuli ataniunga mkono na Gambo atabaki peke yake kwa sababu namjua rais hataki longolongo, kificho wala ubinafsi,” alisema. Alimwomba Magufuli kutambua kuwa Arusha kuna tatizo linalosababishwa na Gambo aliyedai ni mbinafsi, hivyo hawezi kufanya kazi naye kwa sababu kazi za wananchi zinatakiwa zifanyike kwa uwazi. “Niseme kwa mara ya kwanza rais ajue Arusha kuna shida, hatuwezi kuwa na kiongozi ambaye hajielewi, mimi ni meya, natimiza wajibu wangu kama kiongozi wa jamii, nakamatwaje kwa amri yake?  “Kwenye tukio hili niseme nawasifu Jeshi la Polisi wameliweka wazi, nimetoka leo (jana), nimeangalia magazeti na taarifa za polisi, wamesema wao wamepewa agizo na RC, kwa hiyo tulikuwa ndani kwa agizo lake akitaka tumpelekee yeye rambirambi ili yeye azipeleke.  “Sasa msimamo wangu kama meya nasema rambirambi zitakazopitia ofisini kwangu zitaelekezwa kwangu sitazipokea nitawaelekeza wahusika kwa waliofiwa moja kwa moja sitampelekea yeye (Gambo), kwa sababu yeye hakufiwa na huu sio msiba wa ofisi yake,” alisema. Alisema suala jingine linalomfanya asipeleke rambirambi kwa Gambo ni kuwa ni tofauti na tetemeko la ardhi lililotokea mwaka jana mkoani Kagera, ambapo kamati ya kushughulikia maafa hayo iliwekwa wazi na akahoji iweje yeye hakuweka wazi kamati wala akaunti maalumu ya kupelekwa michango hiyo.  “Hakuna utaratibu wa michango, hata ofisi yangu haina maelekezo yoyote kutoka ofisi ya Serikali inayosema fedha za rambirambi zinapelekwa wapi, hatuwezi kupokea maelekezo kwa mtu mmoja tu, yeye amekuwa nani apokee hela za watu agawe?” alihoji. Akizungumzia kauli ya Gambo ya kuwataka viongozi kuacha kuingiza siasa katika msiba huo, alidai kuwa hakuna kiongozi aliyeingiza siasa katika msiba huo kama Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu na yeye hajawahi kufanya siasa kupitia msiba huo.  “Mimi sifanyi siasa, nashukuru kwamba anajiweka wazi, kama kuna mtu amechukulia hili jambo kisiasa ni Gambo na Nyalandu na mliona kuanzia siku miili inaagwa uwanjani alishindwa kunitambua, alikuwa anafanya siasa, hata shughuli hii anavyoiendesha aliiendesha peke yake, kama angekuwa hafanyi siasa angetushirikisha, alizichukua familia na magari ya Serikali kuwapeleka Hoteli ya Mount Meru,” alisema. Pia alisema leo kutakuwa na ibada maalumu ya kuwaombea majeruhi na waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea Mei 6, mwaka huu katika eneo la Marera, Rotia, Wilaya ya Karatu mkoani Arusha na wafiwa kutoa shukrani katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Olasiti na itaongozwa na Askofu Dk. Solomon Masangwa. MTANZANIA Jumapili lilimtafuta Gambo kupitia simu yake ya mkononi ili kutoa ufafanuzi wa madai yaliyotolewa na Lazaro lakini hakupatikana hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno. SABABU YA KUKAMATWA Kuhusu kukamatwa, meya huyo alisema hadi wanaachiwa hajui kosa lililosababisha wakamatwe na kuwekwa ndani kwa siku hizo mbili. Alisema suala la rambirambi ni kwenda kutoa mkono wa pole na kuwafariji wafiwa na si kugawa fedha, bali ni ibada ndiyo maana kulikuwa na viongozi wa dini. “Hadi sasa ninavyoongea sijui kosa na itakuwa ni mara ya kwanza Tanzania inaenda kuweka rekodi ya kutoa rambirambi, tumekuwa tukitoa rambirambi kwenye kata zetu na misiba mingine kwa nini hii iwe nongwa, sijui kesi yangu ni ipi labda nitakaporudi Jumatatu nitaambiwa ila mimi ni Mkristo najua maana ya rambirambi, siwezi kuwaambia watu watume rambirambi kwa njia ya simu, lini rambirambi inatumwa kwa simu. “Nilichojiuliza ni maswali tuliyokuwa tunahojiwa, kwamba kwa nini fedha hizo hazijapitishwa kwa Gambo, kwangu mimi ni jambo ambalo limenisikitisha na Watanzania wajue hakuna kiongozi wa Serikali aliyefariki, walifiwa wananchi wa kata zetu, nimefiwa na wananchi wangu, rambirambi za wananchi zinatakiwa zipelekwe kwa waliofiwa na ndiyo maana siku nne zilizopita nilimtaka Gambo aje hadharani awape rambirambi waliofiwa na alitekeleza. “Sasa kama yeye alikusanya rambirambi akapeleka kwa nini anazuia mimi kupeleka? Tena siyo mimi napeleka, wanapeleka wadau, mimi kazi yangu ni kuratibu  kuhakikisha waliofiwa wanapatikana,” alisema. KAULI YA POLISI Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Yusuph Ilembo, ameliambia MTANZANIA Jumapili kuwa viongozi hao wameachiwa kwa dhamana na kesho wanatakiwa kuripoti polisi.  “Tuhuma ni zilezile za juzi, huwezi kuzuia watu kufikiri wanavyotaka, hao wameambiwa tuhuma zao na wameachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti Jumatatu,” alisema. Juzi alisema walipata maelekezo kutoka kwa Gambo kuwa kuna mkusanyiko, hivyo wao kama polisi wakaenda kuwakamata na kuwahoji na kuhusu kukamatwa kwa waandishi wa habari 10 waliokuwa wakifuatilia tukio hilo, alisema walichukuliwa kimakosa ndiyo maana waliachiwa.
3
SAKATA la uuzwaji wa Kampuni ya Simu ya Airtel iliyokuwa ikiendeshwa kwa ubia na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) limezidi kuchukua sura mpya, huku kigogo aliyeuza kampuni hiyo akiwekwa hadharani. Kutokana na hali hiyo TTCL imetoa msimamo ikiwataka waliouza kampuni hiyo kwa ‘dili’ kuirejesha mikononi mwao kwa hiari badala ya kusubiri nguvu itumike. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL,  Omary Nundu ameitaka Airtel kukabidhi mali za kampuni hiyo kwa TTCL ambayo ndiyo wamiliki halali kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria. Nundu ambaye pia aliwahi kuwa Waziri wa Uchukuzi katika Serikali ya awamu ya nne, ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Rais Dk. John Magufuli kumtaka Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango, kufuatilia kwa karibu umiliki wa kampuni hiyo kabla ya mwaka huu kuisha kwa kuwa taarifa alizonazo kampuni hiyo ni mali ya TTCL. Alisema Kampuni hiyo ya Airtel ambayo ilisajiliwa Novemba 3, 1998 na uongozi wa TTCL kwa mtaji wa Sh bilioni 200 kwa jina la Cellnet iliuzwa kijanja na waliokuwa viongozi wa bodi ya TTCL. Alisema kupatikana kwa kampuni hiyo ambayo ilikuwa chini ya TTCL kulitokana na kuvunjwa na kugawanywa Shirika la Posta na TTCL  Desemba 1993. Alisema baada ya mgawanyiko huo TTCL ikawa kampuni ya Serikali ikiwa na mtaji wa Sh bilioni 200. “Julai 21,1999 baada ya miaka sita thamani ya hisa za TTCL zikapanda kutoka bilioni 200 mpaka bilioni 600, baadae Februari 23, 2001 likaja wazo la kubinafsishwa TTCL akajitokeza mtu anaitwa MSI Cellular Investment ,” alisema Nundu. Alisema mwekezaji huyo alikuja kwa ajili ya kuwekeza katika kampuni ya TTCL katika upande wa simu za mkononi. Alisema katika uwekezaji huo walikubali kutoa  fedha kwa ajili ya  kununulia  hisa ambazo zilikuwa Dola za Marekani milioni 120 ambazo ni sawa na hisa 1,028,665 kati ya  6,000,000. “Kwa  hesabu hii hawa watu hisa zao ni sawa na  asilimia 17.14 si asilimia 35 kama inavyoelezwa, lakini kote wanataja kampuni ina hisa asilimia 35, hili peke yake ni tatizo,” alisema Nundu. Alisema pamoja na hayo katika mchakato huo ulifanyika ujanjaujanja ambapo mwekezaji huyo  hakulipa fedha ambazo aliahidi zipatazo Dola milioni 120, badala yake walilipa Dola milioni 65, huku wakiendelea kuhesabu idadi sawa ya hisa na zile za awali. Alisema siku hiyo hiyo Serikali ikachukua hisa  20,600,650 sawa na asilimia 25 na mwingine akapewa 14,050,000. “Hapo sasa Serikali ndo alikuwa na hisa kubwa kwenye Celtel, watu hao wakachukua hisa nyingine 10,250,000 wakampa mwekezaji ambaye hakujulikana hiyo ndio ikapindua vitabu vya mahesabu, ikawa mwekezaji anahisa 24,626,000,” alisema. Nundu alisema baada ya hapo Celtel ikawa na asilimia 60 na serikali asilimia arobaini na kusababisha bodi ya wadhamini iwe na watu wengi kutoka katika kampuni ya Celtel. Alisema awali kabla ya yote kampuni hiyo ilianza kumilikiwa na mtu asiyejulikana ambaye alikuwa na hisa moja wakati hisa 999 zikiwa za TTCL. Alisema baada ya muda  hisa hiyo moja akapewa mzungu aliyejulikana kwa jina la David Banfod ambaye alizishika kwa niaba ya mtu kabla ya kuzikabidhi kwa Mtanzania (jina linahifadhiwa kutokana na maadili). “Baadae hisa hizo alikabidhiwa Mtanzania kwa bahati nzuri ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya Kampuni za Airtel na TTCL (jina tunalo),” alisema Nundu. Alisema baada ya kukabidhiwa hisa hizo mwenyekiti huyo aliitisha kikao cha wajumbe wa bodi ambapo kati ya wajumbe tisa walihudhuria watano Watanzania wakiwa wanne na raia mmoja wa kigeni. Alisema pamoja na kwamba bodi hiyo ilikuwa na wajumbe tisa lakini kikao hicho cha kuiuza kampuni ya Cellnet kilichokutana Agosti 5, 2005  kilikaliwa na wajumbe watano kikiongozwa na mwenyekiti ambaye alibariki kugawanywa kwa hisa zote na kuipatia  TTCL hisa moja na hisa 99  wakapewa Celtel. Alisema kupitia kikao hicho wajumbe hao walibadilisha mawazo  na kuinyang’anya TTCL hisa ambayo iliwapa hivyo kuifanya Celtel kumiliki kampuni hiyo kwa asilimia mia moja kwa gharama ya Sh milioni 50. Alisema badaaye kikao hicho pia kiliamua kuipa Serikali  hisa asilimia 65 huku TTCL ikiwa haijapewa kitu  na Celtel ikapewa asilimia 35. “Kutokana na mgwanyo huo  gharama za hisa za serikali zikawa Sh milioni 26.6  na wengine wakawa wamechukua hisa za Sh milioni 14.3. Baada ya muda mwenyekiti kwa nafasi yake akachukua hisa nyingine za Sh milioni 10 na kumpatia mwekezaji,” alisema. Alisema pamoja na mlolongo huo wote Juni 23 mwaka huu kampuni ya TTCL iliwataka Kampuni ya Bhart Airtel wajitoe kutoka TTCL, hivyo iliwalipa hisa milioni 14 kama wamiliki wa Airtel ambazo ni sawa na Sh bilioni 40. “Katika hisa hizo walichukua Dola milioni 40 kuongeza mtaji wa Celtel wa kuwanyang’anya fedha zote TTCL na baadae kuamua kuwakopesha tena tena dola milioni 28 nje ya bilioni  40, hizo fedha ziliwekewa riba ya asilimia nane, mpaka leo deni limefika Sh bilioni 76.6,”alisema Nundu. Alisema  mambo hayo yote wameyapata baada ya kuifanyia uchunguzi wa usajili na ubinafsishwaji wa kampuni hiyo wakati wakiwa wanatafuta mtu wakufanya naye kazi. “Sisi tulitafuta tufanye biashara vizuri na wenzetu tukaanza kuchimba ndo tukayaona yote haya tukasema hapa lazima twende tujue mbivu na mbichi kama kuna kulipana tutalipana vipi na tunataka kwenda kistaarabu tu. “Kwa sababu kila ukichimba unakuta mambo mazito zaidi, tumeomba Serikali ilichukue jambo hili sisi interest ikiwezekana ile kampuni ya Celtel turudishiwe,”alisema Nundu. Alisema kampuni ilipata mlolongo wa hasara pale ilipolipwa Dola Milioni 65 ya hisa badala ya Dola milioni 120. “Kampuni hii ilisajiliwa na TTCL, masafa ni ya TTTCL mali zilizotumika kuanzishia kampuni  ni za TTCL hivyo hawawezi kusema ni kampuni yao isipokuwa kipindi hicho kulikuwa na viongozi wasio waaminifu ambao siwezi kuwataja kwakuwa wanajijua wakashiriki kuipora kampuni na kuwapa wageni sasa ni vema wakairudisha kistaraabu,” alisema Nundu. Alisema mchakato uliotumikwa kuipata ni Celtel ni haramu na mpaka sasa ipo kiharamu hivyo ni lazima irudishwe na si kuwapa hisa. Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo kwa Msajili wa Makampuni, inaonyesha kuwa umekuwa ukibalidika tajngu ilipoanzishwa Kampuni ya Celtel Tanzania mwaka 2001 hadi Mei 2005. Kwa wakati huo kampuni hiyo ilikuwa na wakurugenzi wazawa watatu ambapo hadi kufikia Novemba mwaka 2005 aliongezwa mzawa mwingine ambaye kwa sasa ni mbunge mstaafu. Hata hivyo kati ya wakurugenzi hao pia yupo Mtanzania mmoja (jina tunalo) ambaye alipata kufanya kazi  katika taasisi nyeti serikalini. Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba, alisema  menejimenti na wafanyakazi wa kampuni hiyo wanaunga mkono jitihada zinazofanywa na bodi hiyo  ili kuhakikisha haki ya Watanzania inapatikana baada ya kudhulumiwa na wajanja wachache.
3
MBUNGE wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu (pichani) amepongeza dhamira ya dhati na utashi wa Rais John Magufuli wa kuwaletea wananchi maendeleo, kumewafanya wabunge na serikali kuwa ‘jeuri’.Akichangia mjadala wa mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2020/21, Mtaturu alisema utashi wa Rais Magufuli umeifanya serikali kuwa na jeuri ya kupata fedha zinazowezesha utekelezaji wa miradi ya kimakakti ambayo itachangia mabadiliko ya uchumi hapa nchini.“Dhamira ya dhati katika kuhakikisha analeta maendeleo, utashi wake (Rais Magufuli) unatupa jeuri na unaipa jeuri serikali kwa sababu tumekuwa tukipata fedha ya kuweza kutekeleza miradi hiyo, tunaweza kuwa na mipango mizuri lakini isipowezeshwa itakuwa ni kazi bure na itakuwa inabaki kwenye vitabu kama ambavyo tumekuwa tukiona katika baadhi ya maeneo.”“Unaweza kuwa na mpango mzuri lakini ukawa huna fedha lakini ukiwa na mpango mzuri ukiwa ni pamoja na kukusanya mapato inakusaidia wewe kuhakiisha unatimiza malengo,” alisema.Alisema eneo la mianya ya upotevu wa mapato na rushwa ni eneo ambalo lilikuwa linasumbua nchi na kwa Rais kusimama kidedea kupambana na matatizo hayo kunasaidia kupiga hatua na kufanya makusanya ya mapato vizuri. Aidha, pamoja na kushauri serikali kuhakikisha inazidi kuongeza kasi ya kusimamia mapato pia alitaka kuweka kipambele kwa Wakala wa Barabara Vijini na Mijini (Tarura) kupewa fedha za kutosha ili kuvungua vijiji na mikoa kwa barabara na madaraja. yaliyobora.Naye Mbunge wa Tanga Mjini, Mussa Mbarouk (CUF) alisema pamoja na juhudi za wakulima wa Tanzania, kinachowakwamisha ni masoko, jambo ambalo linafanya wengi wao kuishia na umasikini. Kwa upande wa Mbunge wa Geita Vijijini, (CCM) Joseph Musukuma ameitaka serikali kukutana na wamiliki wa viwanda walioshindwa kuviendeleza, lengo kuu likiwa ni kubaini sababu ya viwanda vingi kufa.Alisema kwa kufanya hivyo itasaidia kupata ‘dawa’ ya kusaidia viwanda kuendelea na kufikia Tanzania ya viwanda inayohitajika. Alisema mawazo ya Rais John Magufuli ya kuwanyang’anya wafanyabishara walioshindwa kuviendeleza yalikuwa ni mazuri lakini wasaidizi wake (mawaziri) wangeenda mbali zaidi kwa kuwanyang’anya wamiliki hao mawazo yao.Naye Mbunge wa Jimbo Tarime vijijini (Chadema), John Heche alisema licha ya serikali kuleta mpango huo, lakini kuna baadhi ya miradi ambayo ilikuwa katika mpango huo bado haijatekelezwa.“Mwaka 2009 serikali iliingia mkataba na kampuni moja ya China kwa ajili ya kuendeleza mradi wa Mchuchuma na Liganga, serikali ilitakiwa kumiliki asilimia 20 na hiyo kampuni asilimia 80, na mwaka 2010 mradi ulipaswa kuanza, na thamani ya mradi ni dola za Marekani ni milioni tatu,” alisema Heche na kuongeza: “Mradi huo ungetoa ajira za moja kwa moja 5,000 na za muda mfupi 30,000, tangu mwaka huo hadi sasa hakuna cha mradi.”Mbunge wa Jimbo la Mafinga, Cosato Chumi (CCM) alisema ili serikali ifikie uchumi wa kati ifikapo 2025, inapaswa kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vidogo ambavyo mitaji yake siyo mikubwa. Alisema ujenzi wa viwanda vya sukari ni mzuri na utainua uchumi wa nchi na kuongeza pato la taifa.
3
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harison Mwakyembe amewaalika wajasiriamali wadogo na wakubwa wanaojishughulisha na kazi za utamaduni na sanaa katika tamasha kubwa la bidhaa zitokanazo na Utamaduni na Sanaa la Afrika Mashariki litakalofanyika nchini Septemba 2019, jijini Dar es Salaam.Dk Mwakyembe ametoa mwaliko huo wakati akizungumza kwenye Jukwaa la Fursa za Biashara na Uwekezaji mkoani Lindi leo (Jumanne), wakati akikagua bidhaa za wajasiriamali walioshiriki tukio hilo. Dk Mwakyembe amemwakilisha Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kama mgeni rasmi katika Jukwaa hilo lililoandaliwa na kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) ambayo huchapisha magazeti ya Daily News, HabariLeo, SpotiLeo na mitandao ya kijamii kama Daily News Digital (YouTube), Facebook, Twitter na Instagram.Alisema tamasha hilo ambalo linajumuisha nchi zote za Afrika Mashariki litakuwa na washiriki zaidi ya 100,000 kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki kiasi cha kuwa tamasha kubwa kabisa kuwai kufanyika nchini Tanzania“Tamasha la kwanza lilifanyika Rwanda na lilikuwa na washiriki 17,000 la pili lilifanyika Kenya na kuhudhuriwa na washiriki 45,000 na la mwisho lilikuwa Uganda ambalo liliweza kuwa na washiriki 40,000. Hilo la kwetu ndio funga kazi litakuwa na washiriki zaidi ya 100,000,” alisema Mwakyembe.Aidha, Mwakyembe alisema tamasha hilo litakuwa na mkusanyiko wa wasanii wanaotengeneza sanaa mbalimbali kama vile sanaa za ufundi na sanaa za maonesho na nyininezo.Kwa upande wao wajasiriamali mbalimbali wamefuraishwa na kitendo cha kualikwa na waziri kushiriki katika tamasha hilo wakisema ni fursa adimu kwao ili kuonesha vipaji vyao pamoja na kutangaza kazi za mikono yao.Kikundi cha Tuamke cha Manispaa ya Lindi kikiongozwa na kiongozi wao, Mama Fatma kimesema kimepokea mwaliko huo kwa mikono miwili na watawasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kupata utaratibu wa namna ya kuwakilisha mkoa nje ya Lindi.
3
SERIKALI imesema upo usalama wa kutosha katika vivuko hasa baada ya kuimarishwa kwa mifumo ya kiusalama na ukaguzi.Aidha, imewasisitiza watendaji wake juu ya umuhimu wa ukusanyaji wa mapato katika vivuko hivyo na kuyataka mashirika na taasisi zote zenye madeni ya zaidi ya Sh bilioni 15 kwa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) kuyalipa ili taasisi hiyo itatue changamoto zinazoikabili. Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eliasi Kwandikwa wakati akifungua Baraza la Wafanyakazi la TEMESA, Dar es Salaam.Pamoja na mambo mengine, alisema lengo la kuimarishwa kwa usalama huo ni kukabiliana na majanga ya ajali zinazojitokeza majini. Alisema hatua hiyo imehusisha mikakati mbalimbali ikiwemo kuunda kamati maalumu ambazo pamoja na shughuli zingine pia zimepewa jukumu la kupita katika vivuko hivyo na kufanya kaguzi na kujiridhisha kuhusu usalama wake.“Kwa hiyo tumekuwa na mikakati mizuri kuhakikisha huduma katika vivuko vyote zinakuwa zenye usalama wa kutosha wa abiria pamoja na mali zao,” alisema Kwandikwa. Aliongeza kuwa serikali haipo tayari kuona ajali za vivuko zikitokea tena na kuleta madhara kwa jamii na taifa kwa kusababisha vifo vya watu na upotevu wa mali. Alisisitiza ukusanyaji mapato katika vivuko hivyo kwa kutumia mashine za mfumo za kisasa za ukusanyaji kodi ili kukuza kiwango cha upatikanaji wa mapato kitakachosaidia kutatua changamoto mbalimbali za TEMESA ikiwemo uhaba wa vitendea kazi, vipuri pamoja maboresho ya karakana zake kote nchini.Naibu Waziri huyo alizitaka taasisi zote zenye madeni kwa wakala huyo kuyalipa haraka iwezekanavyo wakati huu ambapo wanashirikiana na TEMESA kufanya utaratibu wa kuwadai wadaiwa hao ili fedha zitakazopataikana zitumike kutatua changamoto hizo na ka ajili ya shughuli nyingine za maendeleo. Awali, Mwenyekiti wa Baraza hilo la wafanyakazi wa TEMESA, Japhet Maselle, alibainisha kuwa pamoja mafanikio kwa wakala huo, kuna vivuko visivyoweza kujiendesha na ukosefu wa vitendea kazi vya kisasa vinavyoifanya taassi hiyo ichechemee.
3
MIPANGO madhubuti inayoendana na utendaji bora, utoaji huduma bora kwa wananchi, na ukusanyaji mapato umeifanya serikali ya awamu ya tano kufufua na kuimarisha mashirika ya umma ambayo yalikuwa goigoi na sasa yanatoa gawio kwa serikali.Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbas alisema serikali ya awamu ya tano ndani ya kipindi cha miaka mitatu tangu mwaka 2015 ilipoingia madarakani, imefanya mageuzi na mabadiliko na yaliyokuwa ndoto kutimia.Amezitaja baadhi ya taasisi na kampuni za umma ambazo zimeinuka na kujiendesha zenyewe na nyingine kutoa gawio kwa serikali ni TRA, Tanesco, Bodi ya Mikopo, Benki ya TIB na Wakala wa Ununuzi serikalini.Kuhusu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk Abbas amesema imeendelea kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya kodi nchini.“Kwa mujibu wa takwimu za hadi Desemba 31, mwaka jana, ambayo ni nusu ya mwaka wa bajeti, ilikusanya shilingi trilioni 7.99 sawa na ongezeko la ukuaji wa asilimia 2.01. Mwezi Desemba pekee mwaka jana, TRA ilivunja rekodi ya mwaka mzima kwa kukusanya Sh trilioni 1.63,” amesema.Dk Abbas amesema miaka michache iliyopita Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) lilisifika kwa gharama kubwa za uendeshaji na kutegemea ruzuku, lakini tangu serikali hii iingie madarakani limeanza kuwa na ufanisi.“Kati ya mwaka 2014 na 2015, Tanesco ilikuwa ikipokea shilingi bilioni 354 na bilioni 163 mtawalia. Lakini umakini wa serikali ya sasa wa kukata mizizi ya ufisadi ikiwemo kuzima mitambo ya kutumia umeme ghali wa mafuta hatimaye tangu 2016/17 haipokei fedha zozote za serikali,” amesema Dk Abbasi.Amesema mwaka 2015, serikali ilitoa Sh bilioni 354 kwa ajili ya kuendesha shirika hilo na mwaka 2016 fedha zilipungua hadi bilioni 163, lakini hadi sasa shirika hilo halitegemei ruzuku ya walipa kodi kujiendesha.
5
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limekutana na wateja wake wakubwa na wenye viwanda Kanda ya Kati na kutakiwa kutetekeleza ahadi ya serikali kwa Watanzania ya kusambaza huduma ya umeme iliyo bora nchini kote.Mkutano huo uliofanyika jijini Dodoma jana, ulihusisha wawekezaji wenye viwanda katika mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida na kufunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge.Dk Mahenge amesema serikali iliahidi kuwapatia Watanzania huduma ya umeme iliyo bora na yenye uhakika ili kuwakwamua kiuchumi hususan walioko maeneo ya vijijini na kuitaka Tanesco kutekeleza ahadi hiyo kwa kuwekeza katika miradi mikubwa ya uboreshaji wa miundombinu ya umeme.Aliitaja miradi midogo na mikubwa inayoendelea kutekelezwa mkoani Dodoma kuwa ni uboreshaji wa kituo kikubwa cha gridi ya taifa cha Zuzu kinachoongezewa uwezo kutoka kupokea megawati 48 hadi megawati 400 ambao unatekelezwa na serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).Dk Mahenge aliwataka wawekezaji kutumia fursa hiyo ya upatikanaji wa umeme wa uhakika kuwekeza zaidi katika viwanda mbalimbali hasa ikizingatiwa kuwa Dodoma ndio makao makuu ya serikali. “Jiji la Dodoma lina fursa nyingi hivyo ni wakati sahihi wa kuwekeza katika kulijenga jiji,” alisema.Amewakaribisha wadau wote waliohudhuria kikao kazi hicho kupita katika ofisi ya mkurugenzi wa jiji la Dodoma na kupata maelezo ya uwekezaji kwani hali ya umeme mkoani humo ni nzuri.
5
Na MWANDISHI WETU MSANII wa Bongo Fleva, Gigy Money, anayetamba na wimbo wake wa ‘Nampa Papa’, ni miongoni mwa wasanii watakaopanda jukwaani katika tamasha la Tigo Fiesta, litakalofanyika Ijumaa katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Msanii huyo, ambaye alikuwa ‘Video Queen’, kwa mara ya kwanza ametajwa kuwa miongoni mwa wasanii watakaopanda katika jukwaa la Tigo Fiesta jijini Tanga, kutokana na kujizolea umaarufu katika muziki wa Bongo fleva. Mbali na Gigy Money, wasanii wengine watakaopagawisha Tigo Fiesta Tanga ni Mavocal, Chege, Nandy, Maua Sama. Wengine ni Vanessa Mdee, Jux, Ben Pol, Aslay, Rostam, Weusi, Darassa, Lulu Diva, Zaiid, Mimi Mars, OMG, Bright na Nchama. Meneja wa Tigo, wanaodhamini tamasha hilo, William Mpinga, alisema kuwa, hadi sasa tamasha hilo limekuwa burudani tosha kwa mashabiki wa miziki wa Bongo fleva na kwamba wao wataendelea kuwajali wateja wao kwa kuwapa ofa mbalimbali, lakini pia burudani. “Tigo Fiesta 2017 kama ilivyo kauli mbiu yetu ‘Tumekusoma’, tunazidi kuwajali wateja wetu na ndiyo maana tunawasikiliza na kuwapa kile wanachokipenda, ikiwamo burudani kama hii ya kuwashuhudia wasanii wao wanaowapenda,” alisema.
1
Na WAANDISHI WETUN -ARUSHA/MANYARA MVUA zinazoendelea kunyesha nchini zimesababisha madhara katika Mikoa ya Arusha na Manyara. Katika Mkoa wa Arusha, mvua hizo jana zilisababisha shughuli za maendeleo katika Barabara Kuu ya Arusha kwenda Karatu, kusimama kwa muda, baada ya kingo za daraja linalounganisha Mji wa Mto wa Mbu na Makuyuni kusombwa na mafuriko. Kutokana na hali hiyo, abiria wanaotoka na kwenda mkoani Mara, watalii wanaotembelea Hifadhi za Manyara, Serengeti, Ngorongoro pamoja na wananchi mbalimbali, walijikuta katika wakati mgumu wa kuendelea na shughuli zao za kila siku kutokana na ubovu wa barabara hiyo. Kukatika kwa daraja hilo ambalo ni kiungo muhimu cha shughuli za maendeleo, kulisababishwa na mvua kubwa iliyonyesha maeneo ya milimani, wilayani Monduli na kusababisha magari zaidi ya 300 kushindwa kupita kwa wakati. Akizungumzia athari hizo kwa njia simu, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Arusha, Mgeni Mwanga alisema baada ya uharibufu wa barabara hiyo, wamefanikiwa kuweka kifusi katika eneo hilo na magari yalianza kupita, kuanzia jana saa sita mchana. “Usiulize ukiwa mbali, njoo hapa ‘site’ uone kwa macho yako kama kweli kuna daraja limesombwa na mafuriko kama unavyouliza. “Kimsingi, daraja halikukatika ila kingo zake ndizo zimemegwa na maji baada ya maji kujaa kupita kiasi. “Yaani, hivi ninavyozungumza na wewe, tunamalizia kujaza kifusi na magari yote yalishaanza kupita na kuendelea na safari,” alisema Mwanga. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Isack Joseph, aliiambia MTANZANIA kwamba kukatika kwa daraja hilo kulisababisha madhara kwa wananchi wilayani kwake. “Maeneo mengi wilayani Monduli yalikuwa na mvua kubwa sana jana usiku na kwa kuwa wilaya ina maeneo yenye milima, maji yaliteremka kwa wingi kuelekea chini. “Kazi ya kutafuta njia mbadala ili kuruhusu magari na watumia barabara waendelee na shughuli zao, zinafanywa kwa ushirikiano wa TANROADS na halmashauri,” alisema Joseph. Naye Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Iddi Kimanta alisema jitihada za kurudisha usafiri katika hali ya kawaida zilifanikiwa na magari kuanza kupita. Pamoja na hayo, Kimanta alisema Serikali ya Wilaya ya Monduli inaendelea kufuatilia madhara ya mvua hizo na itatoa msaada kwa waathirika pindi utakapohitajika. Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Mtaa wa Olkerein, Kata ya Olasiti mjini Arusha, Daud Safari alisema mvua hiyo iliyokuwa na upepo mkali iliezua mapaa ya nyumba na kanisa. Wakati hali ikiwa hivyo mkoani Arusha, mkoani Manyara, wilayani Kiteto nako mvua zilikata mawasiliano ya barabara kati ya Wilaya za Kiteto na Wilaya za Kongwa, Chemba na Kondoa, mkoani Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magesa, aliambia MTANZANIA kwamba Serikali ya wilaya yake kupitia TANROADS, wamejipanga ili kukabiliana na madhara yatakayosababishwa na mvua hizo.
3
UONGOZI wa timu ya soka ya Yanga umesema kuwa malengo yao katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi ni kutwaa taji hilo.Meneja wa timu hiyo, Abeid Mziba aliyasema hayo jana katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika ofisi za Shirikisho la Soka la Zanzibar, ZFF, Amaan mjini hapa.Alisema kuwa wamekuja vizuri na kikosi kilichokamilika kitakachoweza kutoa ushindani, baada ya Jumamosi kutoka sare ya 2-2 na maasimu wao wakubwa, Simba katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga inashuka dimbani leo usiku kucheza na Jamhuri katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Amaan.“Jamhuri ni ndugu zetu tunawaheshimu na udugu tutauweka pembeni, tutapambana ili tutoke na ushindi na kuweza kusonga mbele, “ alisema Mziba. Akizungumzia kuhusu mtindo wa mashindano ya Mapinduzi mwaka huu, ambao ni wa mtoano, alisema sio mbaya lakini ubaya wake unatokea pale ambapo umefungwa mapema. “Mtoano ni mzuri Ila ubaya wake ni pale unapotolewa hivyo tutahakikisha tunasonga mbele, “ alisema.Kwa upande wake nahodha wa Jamhuri, Mohammed Juma Mohammed, alisema kuwa wamejiandaa kwenye mchezo wao huo wa leo na timu yao ipo katika ari nzuri na wanatarajia kushinda. Hatahivyo, alisema kuwa wamejipanga kutoa matokeo mazuri isipokuwa mchezo ni mchezo na lolote linaweza kutokea, lakini wamejiandaa kwa ushindi.Aidha, alisema kuwa ni kweli mwaka jana walifungwa mabao mengi, lakini haimaanishi kama ni wateja wao ila ni matatizo tu ya wachezaji kushindwa kufuata maelekezo ya kocha.Naye kocha wa timu ya Jamhuri, Mustafa Seif Suleiman alisema kuwa wamejiandaa vizuri ili waweze kupambana na Yanga na dakika 90 ndizo zitakazotoa matokeo ila wamejiandaa vizuri ili waweze kushinda. Katika mashindano hayo mwaka jana timu hizo zilipangwa kundi moja, ambapo Yanga iliibuka na ushindi mnono wa mabao 6-0.
4
SEKRETARIETI ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), imekutana kujadili namna wanavyoweza kuboresha usimamizi wa sheria, kufanya utafi ti na namna ya kutoa elimu itakayosaidia kuzuia biashara haramu ya usafi rishaji wa binadamu.Katika warsha ya siku nne iliyoanza jana jijini Dar es Salaam na kukutanisha Kamati za kiwizara za nchi wanachama kutoka mataifa 16 ya jumuiya hiyo, wamepanga kuweka mpango madhubuti wa kutoa elimu, kusaidia waathirika na watoa taarifa za biashara hiyo, kufanya utafiti na kupeana taarifa pamoja na kusimamia sheria zinazokataza biashara hiyo haramu duniani.Akifungua warsha hiyo, Ofisa Mwandamizi wa Teknolojia ya Hawari na Mawasiliano (Tehama) wa Sekretarieti ya SADC, Robin Unuth alisema biashara hiyo haramu bado imekuwa ikikwamisha usalama ndani ya SADC na kwamba sheria za kukabiliana na changamoto hiyo zinapaswa kutumiwa ipasavyo, huku utaratibu wa kimawasiliano ulio bora ukitafutwa ili kuuondokana na biashara hiyo.“Sheria zipo, zinapaswa kufuatwa lakini hazitoshi, kamati za kiwizara za nchi wanachama zilikutana kujadili kuhusu jinsi gani zitashirikiana kukabiliana na changamoto hizo kwenye mkutano uliofanyika Julai mwaka, Kwenye mkutano huo, tulipanga kuweka mpango madhubuti kutoa elimu, kusaidia waathirika na watoa taarifa, kufanya utafiti na kupeana taarifa pamoja na kusimamia sheria zinazokataza biashara hiyo haramu duniani na sasa tunataka kuona ni kwa njia gani tunaweza kutekeleza mipango na tafiti hizo kwenye nchi mbalimbali,” alisema.Mkurugenzi wa Idara ya Ushiriano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Innocent Shiyo alisema kuwa warsha hiyo inaangalia zaidi biashara haramu ya binadamu kama miongoni mwa biashara haramu duniani kwa sasa. Alisema, “Kuna biashara kuu tatu haramu kubwa zaidi duniani nazo ni biashara ya silaha, dawa za kulevya na biashara ya binadamu.Kwa upande wake, Katibu wa Sekretarieti ya Kuzuia Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu, Seperatus Fella alisema kuwa warsha hiyo imewakutanisha viongozi na maofisa kutoka mataifa mbalimbali ili kuweka nguvu katika kuhakikisha kuwa biashara hiyo haramu inatokomea. Naye, Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Biashara ya Binadamu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(DRC), Ditunga Joseph alisema nchini kwake kuna changamoto kubwa ya biashara ambayo imekuwa ikichangiwa na kukosekana kwa amani.
3
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema magari yanayobeba kemikali za kulipuka yanatakiwa kupata kibali cha Mkemia Mkuu wa Serikali na si kibali kutoka kwa Wakala wa Barabara (Tanroads).Kamwelwe amesema hayo mwishoni mwa wiki mjini Dodoma wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo sekta ya ujenzi.Amesema ameona atoe ufafanuzi huo kutokana na mkanganyiko uliopo wa utoaji wa vibali.Waziri huyo amesema kuna sheria wanazotekeleza lakini kuna mkanganyiko juu ya gari linalobeba kemikali za kulipuka zinapewa kibali na mkemia mkuu wa serikali na si Tanroads na magari hayo hayawezi kupita kwenye mizani kama huna kibali cha mkemia."Pia nataka wahusika kwenye wizara yangu watoe ufafanuzi magari yanayobeba milipuko yanapimwa au hayapimwi kwenye mizani,” amesema.Pia amesema kuna sheria ya uzito wa magari na sheria hizo watazipitia na kutoa maelekezo.Waziri huyo amesema ripoti ya miradi ya wizara hiyo iliyopitiwa na kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu imeonekana kuwa na upungufu mwingi.Kamati ya Bunge ya miundombinu ilipitia mradi wa ujenzi wa viwanja vya ndege jijini Dodoma, Dar es Salaam na mradi wa barbara mkoani Mtwara.Alisema amepewa taarifa na kamati hiyo kuwa ripoti hiyo ni mbaya haina ufanisi wowote kulingana na miradi hiyo.Alitoa siku moja ili ripoti hizi ziandikwe upya kutokana na kuhofia kushambuliwa na wabunge kutokana na ripoti hiyo. Hata hivyo, alisema wanatakiwa kwenda kukesha ili kuhakikisha wanabadilisha ripoti hizo."Naomba leo msilale hakikisheni mnamaliza hiyo ripoti," alisema Kamwelwe.Alisema hakuna kilichofanyika kutokana na kwamba kamati hiyo imeiponda sana hiyo ripoti. Pamoja na hayo alilitaka Baraza hilo kutoa matokeo chanya kwani dhana ya Baraza mahali pa kazi ni ushirikishwaji.Alisema madhumuni ya baraza ni kutoa fursa kwa watumishi juu ya masuala yanayohusu maslahi yao.Katibu Mkuu wa wizara hiyo sekta ya ujenzi, Elius Mwakalinga alitaka kila mshiriki alitendee haki Baraza hilo kwa kutoa mchango ambao utakuwa na tija na wenye lengo la manufaa.Pia alisema wamejipanga kuwajengea uwezo wataalamu ili wawe mahiri. Pia kuboresha mifumo ya magari ili kuepuka foleni kwenye vituo vya mizani.
3
Na LEONARD MANG’OHA -DAR ES SALAAM WATU sita, akiwamo Mwenyekiti wa Mtaa wa Mbezi, ambaye ni Imamu wa Msikiti wa Huda Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam, wametiwa mbaroni baada ya kukamatwa na meno 28 ya tembo, yenye uzito wa kilogramu 377. Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, alisema watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 13 na 14, mwaka huu, huko Mbezi Beach, wakiwa wameyahifadhi meno hayo kwenye ghala. Waziri Maghembe alimtaja mwenyekiti huyo kuwa ni Bakari Seruni, wengine ni Mohamed Yahaya, Juma Jebo, Hamisi Omari, wote wakazi wa Dar es Salaam, Amiri Shelukindo, mkazi wa Gairo, mkoani Morogoro na Ahmed Bakari, mkazi wa Mkuranga, Pwani. Alisema kati ya meno hayo, 21 yalikutwa yamefichwa kwenye ghala, mengine  saba yalikuwa yamehifadhiwa nyumbani kwa mmoja wa watuhumiwa hao. “Jana usiku mmoja wao alituambia tusimsumbue mke wake ili tumwambie atuonyeshe meno ambayo yamefichwa ndani, ndiyo tukafanikiwa kuyakamata hayo meno saba. “Wataalamu wameyapima meno haya yanaonesha hawa tembo wameuawa kama miaka mitatu iliyopita, kwa hiyo inaonesha kuwa waliua tembo wengi wakatunza mzigo nyumbani, sasa wanatafuta wanunuzi,” alisema Profesa Maghembe. Aliwataka wale wanaojihusisha na uwindaji haramu, ikiwamo wa tembo na faru kuachana na kazi hiyo na kufikiria kazi nyingine, kwani kuendelea na kazi hiyo kutawafanya kwenda jela kwa miaka isiyopungua 25. Aliongeza kwamba, pamnoja na China kupiga marufuku biashara ya meno ya tembo nchini humo, bado biashara hiyo inashamiri katika mitandao mbalimbali, hali inayochangia kukwamisha mapambano dhidi ya ujangili wa tembo na ndovu katika maeneo mbalimbali duniani.
3
“Hatujapata taarifa rasmi hivyo siwezi kuzungumzia suala hilo, nasubiri watakapotuletea taarifa, basi tutafuatilia suala zima na kushauriana nao kwanza,” alisema Mwesigwa. Mwesigwa alisema kimsingi pande mbili zinapoingia mkataba, inapofika hatua ya kuvunja upande mmoja hauwezi kuamua wenyewe, lazima upatikane upande wa tatu, ili kuonyesha juhudi za kulitatua suala zilifanyika”.“Mfano wa ndoa, wanaingia wawili, lakini mmoja huwezi kusema basi imetosha, lazima zifanyike juhudi, kwa hiyo mimi nadhani pande zote bado zina nafasi ya kufanya juhudi za kuokoa hii kitu,” alisema Mwesigwa.Pia Mwesigwa alisema suala hilo litakapofika kwao au likipelekwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kote huko lazima Yanga ikaoneshe juhudi ilizofanya kutatua kabla ya kuvunja mkataba.Desemba mwaka jana Yanga ilitangaza kuvunja mkataba na kiungo wake huyo raia wa Rwanda kwa madai ya utovu wa nidhamu zinazoiathiri timu yao. Aidha Yanga ilisema licha ya kuonya tabia hiyo hasa ya kuchelewa kurudi anaporuhusiwa kwenye kwao, Niyonzima amekuwa akirudia jambo hilo mara kwa mara.Pia Niyonzima anatuhumiwa kushiriki katika mashindano ambayo sio rasmi na bila kuruhusiwa na klabu akiweka maslahi yake mbele ameshindwa kuishi kwa kufuata vipengele vya mkataba wake na kumtaka kulipa dola za Marekani 71,175 (milioni 143) kama gharama za kuvunja mkataba na kwamba watapinga usajili wake popote kama hawatalipwa fedha hizo.
4
HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam itaanza kutoa elimu kwa jamii kuhusu athari za mifuko ya plastiki kwa kutumia mfumo wa matangazo ya umma katika Manispaa zake zote kuanzia Ijumaa.Mkuu wa Idara ya Udhibiti Taka na Hifadhi ya Mazingira wa Jiji la Dar es Salaa, Shedrack Maximilian alieleza hayo alipozungumza na gazeti hili kuhusu zuio la serikali la matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia Juni Mosi, mwaka huu.Alisema Jiji la Dar es Salaam linalokadiriwa kuwa na watu milioni sita lina shughuli nyingi, zikiwemo za viwanda na biashara hivyo limeathirika kwa kiasi kikubwa na mifuko ya plastiki.“Kuanzia Ijumaa Jiji litaanza kutoa elimu kwa kutumia magari. Yatatolewa matangazo kwenye maeneo yote ya Jiji lakini vile vile kutakuwa na kikao wiki ijayo cha wataalamu wa mazingira wa Manispaa ili na wao waweke mipango ya namna ya kutoa elimu ya madhara ya mifuko ya plastiki,“ alisema Maximilian.Alisema wananchi wa Jiji la Dar es Salaam wanapaswa kuwa wa kwanza kupinga matumizi ya mifuko ya plastiki kwa sababu inaleta athari nyingi, zikiwemo kuziba mifumo ya majitaka hivyo kusababisha mafuriko na pia kuathiri viumbe hai wa baharini.“Mifuko ikiishaingia kwenye bahari inaharibu idadi ya samaki. Kama dunia haitazuia mifuko ya plastiki itafikia hatua mifuko ya plastiki kwenye vyanzo vya maji na mazalia ya samaki itakuwa ni mingi kuliko hata samaki wenyewe.“Wananchi waanze sasa kuzoea kutumia mifuko mbadala. Miaka ya tisini hii mifuko ya plastiki haikuwepo, ilikuwa ikitumika hiyohiyo mifuko mbadala na vifaa mbadala,” alisisitiza Maximilian.Alisema mifuko mbadala ya kubeba bidhaa kama vile magunia, ndoo na sufuri bado ipo na kwamba kinachotakiwa ni mabadiliko ndani ya jamii.Hivi karibuni Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira, ilipiga marufuku uzalishaji, uuzaji, usafirishaji nje ya nchi, usambazaji, uuzaji na matumizi ya mifuko ya plastiki ifikapo Juni Mosi, mwaka huu.Kwa mujibu wa katazo hilo adhabu za faini au vifungo zitahusika kwa atakayekiuka katazo kulingana na kanuni za marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki za mwaka 2019 zilizoandaliwa chini ya Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004.Faini zitakazotozwa ni pamoja na Sh milioni 20 kwa kuingiza nchini mifuko ya plastiki, Sh milioni 20 kwa kusafirisha nje ya nchi, Sh milioni 10 kwa kuzalisha, kuhifadhi na kusambaza, Sh 10,000 kwa kuuza na Sh 30, 000 kwa kutumia mifuko ya plastiki.Katazo hilo pia linasema bidhaa ambazo hazitaathiriwa na katazo hilo ni pamoja na vifungashio vya dawa, vyakula kama vile maziwa, korosho, bidhaa za viwandani,
3
Na Said Salim –  dar es salaam SHIRIKA la Afya la Kimataifa (WHO) limeitaja Tanzania kushika nafasi ya 14 katika orodha ya nchi zinazoongoza kwa unywaji pombe barani Afrika kati ya nchi 46 zilizofanyiwa utafiti mwaka 2016. Kwa mujibu wa ripoti ya WHO ya hali ya kiafya kulingana na viashiria vya malengo endelevu ya milenia (SDG) ya mwaka jana, Tanzania ni ya nne miongoni mwa nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kati na ya 49 duniani. Ripoti hiyo inaonyesha kuwa wakati wa utafiti huo, kiwango cha pombe halisi kinachonywewa na Mtanzania mmoja mmoja mwenye umri wa kuanzia miaka 15 na kuendelea, kilikuwa lita 6.3 kwa mwaka. WHO imesema kuwa ripoti hiyo imeandaliwa kwa kutumia takwimu zinazozalishwa na kuhifadhiwa na shirika hilo au mashirika mengine ya kimataifa ambayo ni mwanachama. Katika ukanda wa Afrika Mashariki, Uganda ndiyo inayoshika nafasi ya kwanza ikiwa na wastani wa unywaji wa lita 11.8 kwa mtu mmoja mmoja kwa mwaka ikifuatiwa na Rwanda (lita 11.5), Burundi (6.9) na Kenya ni ya tano kwa lita 4.4. Mbali ya kuongoza Afrika Mashariki kwa kuwa na kiwango kikubwa cha unywaji pombe, Uganda pia imeshika nafasi ya kwanza Afrika na ya 11 duniani ikilingana na Namibia, huku Mauritania na Libya zikiwa na kiwango kidogo kuliko nchi zote duniani cha lita 0.1 kwa mwaka. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Lithuania ndiyo inayoongoza kwa kiwango cha unywaji pombe duniani, ikiwa na wastani wa lita 18.2 ikifuatiwa na Belarus lita 16.4, Jamhuri ya Maldova (lita 15.6) na Urusi lita 13.9. Miongoni mwa nchi zilizoendelea zaidi kiuchumi (MEDCs), Ujerumani inashika nafasi ya 15 duniani ikiwa na wastani wa lita 11.4, Denmark nafasi ya 23 (lita 10.1), Uswisi nafasi ya 24 sawa na Canada (lita 10.0), Marekani nafasi ya 27 (lita 9.3) na Uholanzi nafasi ya 33 (lita 8.7). Akizungumzia na Mtanzania kuhusu takwimu hizo za WHO, Mtanzania anayefanya PHD ya udaktari katika Chuo Kikuu cha Udaktari Tokyo cha Japan, Dk. Isaac Maro, alisema ingawa kiwango cha unywaji pombe kwa Tanzania kimeonekana kuwa ni kidogo kuliko nchi nyingi za Afrika Mashariki, bado ni kikubwa kwa wastani, hivyo kinapaswa kupunguzwa ikizingatiwa kuwa pombe ni hatari kwa afya ya binadamu. “Unywaji wa pombe uliokithiri unatambulika kuwa moja ya sababu ya maradhi mengi yasiyo ya kuambukiza kama vile maradhi ya mfumo wa damu (shinikizo la juu la damu na maradhi ya moyo) pamoja na maradhi ya mifumo kama vile kisukari. “Takwimu hizo zimeonyesha kuongezeka kwa kiwango cha maradhi haya miongoni mwa Watanzania ambapo Watanzania 33,064,128 walionekana kuhitaji ushauri au matibabu dhidi ya maradhi yasiyo ya kuambukiza kwa mwaka 2015. “Utafiti huo pia ulionyesha kuwa uwezekano wa kufariki kutokana na maradhi yasiyo ya kuambukizwa pamoja na saratani kwa Watanzania walio na umri wa kati ya miaka 30 na 70 ulikuwa asilimia 17.8 kwa mwaka 2016,” alisema Dk. Maro anayefanya kipindi cha Afya Check na Clouds Media. Machi 15, 2016, Rais Dk. John Magufuli wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa wapya, aliwataka viongozi hao  kuhakikisha vijana wanaacha vitendo vya unywaji pombe, mchezo wa pool na michezo mingine wakati wa saa za kazi kama mkakati wa kuhakikisha kila Mtanzania anashiriki shughuli ya uzalishaji mali katika eneo lake. Kauli hiyo ya Magufuli iliungwa mkono na wakuu wa mikoa mbalimbali kwa kuendesha operesheni za kuwakamata watu waliokuwa wakinywa pombe saa za kazi na kuwachukulia hatua za kisheria. Katika kupunguza matumizi ya pombe nchini, Februari 16, mwaka jana, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alitangaza amri ya Serikali kupiga marufuku matumizi ya pakiti za plastiki kufungashiwa pombe kali maarufu kwa jina la ‘viroba’ kuanzia Machi mosi, mwaka jana. “Sasa hivi viroba vimeenea kila kona, hata watoto wa shule za msingi wanatumia kwa sababu ni rahisi kuweka mfukoni na kutembea navyo. Kuanzia tarehe moja Machi, tutakayemkamata ameshika pombe ya viroba, sisi na yeye,” alisema. Majaliwa alikuwa akikazia kauli ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla, aliyoitoa bungeni mjini Dodoma Februari 7, mwaka jana. Katika mkutano huo wa Bunge, wakati akijibu hoja za wabunge waliokuwa wakilalamikia kilevi hicho kinavyopunguza nguvu kazi ya Taifa, Dk. Kigwangalla alisema Serikali iliamua kupiga marufuku kutengenezwa au kuingizwa nchini kwa viroba pamoja na kuziba mianya yote ya uingizaji wa kilevi hicho kwa sababu kilikuwa kikiharibu nguvu kazi ya Taifa. Miongoni mwa wabunge waliolalamikia viroba ni pamoja na Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Esther Matiko ambaye alilieleza Bunge kuwa pombe hiyo inasababisha vifo vya vijana wengi nchini ambao ndio tegemeo kubwa na nguvu kazi ya Taifa. “Katika kipindi hiki kifupi cha likizo yangu, nilikuwa jimboni kwangu na tumezika vijana wanne waliofariki kwa matumizi ya viroba. “Hivyo wananchi wa jimbo langu wameniagiza kuja kulieleza Bunge athari za pombe hiyo ili tuweze kujadili na kuona namna gani ya kuliokoa Taifa, hasa vijana kutoka katika janga hilo,” alifafanua Matiko.  
3
UPANDE wa utetezi katika kesi ya utakatishaji fedha inayomkabili aliyekuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na wenzake umepinga mahakama kupokea nyaraka zilizotumika kuingiza nyasi bandia na nyaraka za kuomba msamaha wa kodi zilizopelekwa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na klabu hiyo.Wakili wa Utetezi, Nehemiah Nkoko alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba. Awali, Mchunguzi Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Frank Mkilanya alidai nyasi hizo zilinunuliwa kwa wakala anayeitwa Hamisi na zilitoka katika Kampuni ya Nina iliyopo China.Alidai wakati wa uchunguzi, alimhoji Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa klabu hiyo, Zacharia Hans Poppe ambaye alidai Hamisi alifariki na akampa cheti cha kusafirishia mwili ambacho aliomba kukitoa kama kielelezo. Wakili wa Serikali, Leonard Swai aliomba kutoa kielelezo hicho mahakamani ili kitumike kama ushahidi. Hata hivyo, Wakili Nkoko alipinga kupokewa kwa kielelezo hicho kwa madai kwamba si nakala halisi na kinachothibitisha kifo ni cheti cha kifo.Alidai kwa mujibu wa sheria ni lazima shahidi aseme kwamba nyaraka halisi iko wapi. Akitoa uamuzi Hakimu Simba alikubaliana na hoja za upande wa utetezi na kukataa kupokea kielelezo hicho.Akiendelea na ushahidi, shahidi huyo alidai katika uchunguzi, alibaini viongozi wa Klabu ya Simba walipeleka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) nyaraka ikionesha nyasi walizinunua kwa zaidi ya Dola za Marekani 40,000 lakini alipohoji aliambiwa walinunua kwa Dola za Marekani 109,000.Alidai viongozi hao walipotakiwa kupeleka nyaraka TBS ili wapate msamaha wa tozo ya ukaguzi wa mzigo walipeleka nyaraka ya Dola za Marekani 40,000. Shahidi alidai mzigo huo haukufanyiwa ukaguzi China hivyo walitakiwa kulipa gharama lakini kutokana na barua waliyoandika TBS walisamehewa.Alidai aliitaarifu TRA kuhusiana na nyaraka hizo. Baada ya kudai hayo, aliomba kutoa nyaraka hizo kama kielelezo mahakamani lakini mawakili wa utetezi walipinga wakidai hana mamlaka ya kutoa kielelezo hicho. Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 28 mwaka huu kwa ajili ya kutoa uamuzi mdogo kuhusu mapingamizi hayo.
4
KOCHA wa Simba, Patrick Aussems amesema walilazimika kubadili mbinu za uchezaji ili kupata matokeo mazuri katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya African Lyon, ambao walishinda 3-0 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.Akizungumza baada ya mchezo huo, Aussems alisema uwanja haukuwa rafiki ndio maana walikuja na mbinu nyingine iliyowasaidia kupata matokeo hayo.“Tunashukuru tumepata pointi tatu, inamaanisha kila mtu anatimiza wajibu wake vizuri, tumeonesha jitihada zetu na kupata ushindi na sasa tunaangalia mchezo ujao,” amesema.Wekundu hao waliingia na mbinu ya kucheza mipira mirefu tofauti na walivyocheza michezo iliyopita walitumia zaidi mipira ya pasi hadi kufika golini.Hata hivyo, amesema matokeo hayo yameshapita na mawazo yao kwa sasa ni mchezo ujao dhidi ya Azam FC utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kesho.Kutokana na umuhimu wa mchezo huo, Kocha huyo aliwapumzisha nyota wake wengi wa kikosi cha kwanza katika mchezo uliopita dhidi ya Lyon na kuwapa nafasi wale waliokuwa hawatumiki sana.
4
Na Dennis Luambano – Same WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba, amesema anakusudia kulitangaza eneo la Ndolwa lililopo Kata ya Mamba Myamba, Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, kuwa ni hatarishi na kuwataka wananchi wanaoishi kuhama na kuacha shughuli za kibinadamu.  Kusudio hilo alilitangaza mjini hapa jana baada ya kuombwa na Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule, kutokana na kuwapo kwa dalili za awali na hatarishi za kutokea maporomoko ya ardhi katika eneo hilo.     January aliyetembelea wilaya hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira, alisema watalitangaza kama eneo linalolindwa kwa mujibu wa sheria ya mazingira kifungu cha 51 na 52. “Tumeamua tutalitangaza rasmi kama ni eneo hatarishi. Watu wa NEMC (Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira) watafanya tathmini ya kitaalamu ya athari ya mazingira kisha nitalitangaza katika Gazeti la Serikali. “Hatutaki kuona maafa yanatokea kwa mara ya pili katika eneo hilo,” alisema January. Licha ya kusudio la kulitangaza, pia alisema watazingatia utashi wa wananchi wanaoishi katika eneo hilo ili kuepusha migogoro.
3
KUTOKANA na umeme wa maji (Hydro power) kuwa wa gharama nafuu zaidi ikilinganishwa na unaotokana na vyanzo vingine, Serikali imepongezwa kwa kulinda vyanzo vya maji. Akizungumza hivi karibuni, Naibu Mkurugenzi wa Tanesco anayeshughulikia uzalishaji, Mhandisi Abdallah Ikwasa, alisema matumizi ya juu ya umeme nchini kwa sasa ni megawati 1,060. Alisema kati ya hizo, Tanesco kwa kutumia mitambo yake, huzalisha megawati zaidi ya 1,000 ambazo megawati 381 zinatokana na umeme unaozalishwa kutokana na maji, kutoka katika vituo vya Kidatu, Mtera, New Pangani Falls, Hale na Nyumba ya Mungu. Alisema katika siku za hivi karibuni, shughuli za kibinadamu zimekuwa zikiongezeka kwenye vyanzo vya maji na kuathiri vituo vya kufua umeme na hata kutishia uzalishaji. Ikwasa alitoa mfano Mto Pangani ambako yapo maeneo ambayo shughuli za kilimo zinaendelea karibu na mto, na madhara yatokanayo na shughuli hizo husababisha kingo za mto kuwa dhaifu na wakati wa mvua maji yanachukua udongo na kuingiza kwenye mto na hivyo kina kinakuwa kifupi. Kwa habari zaidi jipatie nakala yako ya MTANZANIA.
3