text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
BARAZA la Habari Tanzania (MCT) limesema jumla ya wanahabari 81 watachuana katika kinyang’anyiro cha kuwania Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) mwaka huu.Katika kinyang’anyiro hicho, waliojitokeza ni pamoja na waandishi wanawake 34, ikiwa ni ongezeko kubwa tofauti na mwaka jana ambako walikuwa 24, huku walioingia katika kinyang’anyiro hicho wakiwa ni pamoja na waandishi wa habari wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) wachapishaji wa Daily News, HabariLeo na SpotiLeo, Frank Leonard, Rahel Palangyo, Lasteck Alfred, Abdallah Msuya na Adam Lutta.Akizungumza wakati akitangaza tuzo hizo, Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga alisema kutangazwa kwa tuzo hizo kunaokana na kukamilika kwa kazi ya kupitia na kuchagua zile zilizo na ubora zaidi iliyofanywa na jopo la majaji saba lililokaa kuanzia Juni 13 hadi Juni 19, mwaka huu.Mukajanga alisema kuna ongezeko la wateule kwa upande wa runinga ambapo wapo wateule 20 kutoka wateule 15 katika tuzo za 2017 na pia kuna ongezeko kwa wateule upande wa redio kutoka 11 hadi 20, ongezeko hilo pia lipo kwa upande wa magazeti ambapo mwaka 2017 lilikuwa na wateule 19 ukilinganisha na 46 wa sasa.Makundi yaliyoshindanishwa ni tuzo ya uandishi wa habari za biashara, uchumi na fedha, habari za michezo na utamaduni, afya, kilimo na biashara za kilimo, elimu, utalii na uhifadhi, kodi na mapato, uchunguzi, data, haki za binadamu na utawala bora, mpiga picha bora, mpigapicha bora wa runinga, katuni bora, habari za jinsia na vijana, habari za wazee, habari za watoto, gesi, mafuta na uchimbaji madini, usalama na ubora wa chakula, dawa na vipodozi, kundi la wazi, na usalama barabarani.Mwenyekiti wa Majaji wa tuzo za EJAT, Kiondo Mshana alisema inasikitisha waandishi wamepoteza mwelekeo kwenye habari za uchunguzi ambazo wamekuwa wakiziandika juu juu na kutofika mwisho, zikiwa hazina kichwa wala miguu.
3
RIBEIRA, PORTO MLINDA mlango wa klabu ya Porto, Iker Casillas, amesema amekuwa na furaha kubwa ya kuifunga Chelsea na si kumfunga kocha wake wa zamani Jose Mourinho. Awali wawili hao waliwahi kufanya kazi pamoja katika klabu ya Real Madrid, lakini Casillas anaamini kuwa kiwango chake kilishuka kutokana na tabia ya kocha huyo kumuweka benchi katika michezo mbalimbali. Hata hivyo, Casilas mwanzoni mwa Septemba alisema Mourinho amemfanya thamani yake ishuke katika soka hivyo hana uhusiano mzuri na kocha huyo, lakini katika mchezo wa juzi wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya ulikuwa wa kwanza kuwakutanisha wawili hao. Katika mchezo huo wa juzi Chelsea ilijikuta ikiambulia kichapo cha mabao 2-1 na kumfanya mlinda mlango huyo kuwa na furaha kubwa kutokana na ushindi huo. “Sina furaha kwa sababu nimemfunga kocha wangu wa zamani Jose Mourinho, lakini nina furaha kubwa kwa sababu nimeisaidia timu yangu kuipa ushindi. “Sina tatizo na Mourinho na hata kabla ya mchezo niliweza kusalimiana na kocha huyo kwa kushikana mikono, siwezi kukumbuka ya zamani ambayo alinifanyia nikiwa Madrid, kwa sasa ni kuangalia yajayo,” alisema Casillas. Mchezo huo ilipigwa katika Uwanja wa Estadio do Dragao na kuwafanya Porto wafanikiwe kushika nafasi ya pili katika kundi G.  
4
Ajira ni moja ya changamoto kubwa inayowakumba vijana sehemu ya Afrika Mashariki , barani Afrika na dunia kwa ujiumla wake, ambapo changamoto hii kwa sasa inakabiliwa kwa vijana kujiajiri wenyewe.Mradi wa uwajibikaji Zanzibar unaosimamiwa kwa mashirkiano ya jumuiya tatu imejikita katika kuhakikisha vijana wanajiajiri wenyewe ambapo wanatoa elimu ya kujiajiri katika Wilaya tatu za Pemba ambazo ni Wilaya ya Wete,Chake Chake na Micheweni.Jumuiya hizo za Uhifadhi wa Mali asili Pemba NGENAREKO,jumuiya ya waaandishi wa habari za maendeleo Zanzibar,WAHAMAZA na chama cha waandishi wa Habari Tanzania upande wa Zanzibar TAMWA,kupitia mradi wa PAZA wanahakikisha Elimu hio ya kujiajiri kwa vijana inawafikia ili kuweza kujiongezea kipato, ambapo serikali pekee isingeweza kuajiri vijana wote wanaofikia umri wa kuajiriwa.Akizungumza muwezeshaji katika jimbo la Ole Khadija Henock amesema hivi sasa vijana katika Wilaya Chake Chake wamekuwa wakifanya juhudi za makusudi ili kujikomboa kutokana na ukosefu wa ajira ambapo wanafanya shughuli za kilimo,utengenezaji wa sabuni na kazi za mikono kama kushona mikoba ya ukili na kuiremba kwa lengo la kuiongezea thamani .Amesema “kupitia mradi wa PAZA,vijana wamepata mwamko na kuamua kujikusanya kwa vikundi na kuzalisha mali jambo ambalo linawaongezea kipato kwa sasa na kukabiliana na tatizo la ajira”aliongeza. Aidha akizungumza Saidi Ali ambaye ni kijana mwanamichezo amefafanunua zaidi kuwa vijana katika Wilaya ya Chake wamejikita katika ajira ya michezo wa mpira wa miguu pia, ikiwa timu ya vijana hao wa jimbo la Ole walinyakuwa ushindi katika mashindano ya kombe la wilaya ya Chake chake msimu uliopita.
3
Na THERESIA GASPAR-DAR ES SALAAM   MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga jana walirejesha furaha kwa mashabiki wao baada ya kuifanyia mauaji timu ya Ndanda FC ya Mtwara na kuchomoza na ushindi mnono wa mabao 4-0. Yanga waliokuwa wenyeji wa mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, walipania kulipiza kisasi baada ya wapinzani wao kuwabana na kutoka sare ya bila kufungana walipokutana katika mzunguko wa kwanza wa ligi. Matokeo ya ushindi wa jana yameiongezea kasi Yanga na kufanikiwa kupunguza tofauti ya pointi kati yao na vinara wanaoongoza katika msimamo wa ligi hiyo, kwa kufikisha pointi 40 huku Simba wakiwa wamejikusanyia pointi 41. Ushindi wa jana ni wa pili kwa kikosi cha Wanajangwani hao kikiwa chini ya kocha wao mpya Mzambia, George Lwandamina, ambaye alikiongoza walipotoa kipigo cha mabao 3-0 dhidi ya JKT Ruvu kabla ya kulazimishwa sare ya 1-1 na African Lyon. Mshambuliaji Donald Ngoma aliyerejea uwanjani kwa kasi baada ya kukosa mchezo uliopita, aliwanyanyua mashabiki wa Yanga dakika ya nne ya mchezo baada ya kufunga bao la kuongoza kwa kichwa akiunganisha vyema mpira wa kona iliyochongwa na Haruna Niyonzima. Dakika ya 20, Amissi Tambwe, alikuwa katika nafasi nzuri ya kuifungia timu yake bao la pili lakini shuti alilopiga akiwa nje ya eneo la hatari baada ya kupokea pasi ya Emmanuel Martin lilipaa juu ya lango. Ngoma aliyeingia uwanjani akiwa na uchu wa kusaka mabao, aliandika bao la pili kwa timu yake katika dakika ya 21 baada ya kupokea pasi ya Martin ambaye alionyesha makali ndani ya kikosi cha Yanga baada ya kusajiliwa kwenye dirisha dogo. Ngoma alifunga bao hilo baada ya kuachia shuti kali akiwa ndani ya eneo la 18 ambalo lilipitiliza moja kwa moja langoni mwa Ndanda baada ya kipa kuhama kwenye eneo lake. Dakika ya 25, Tambwe alifanikiwa kufunga bao lake ya tisa msimu huu na kulingana na Simon Msuva na Shiza Kichuya wa Simba, baada ya kuwapiga chenga mabeki wa Ndanda na kuambaa na mpira hadi kwenye eneo la hatari na kuachia shuti lililotinga moja kwa moja nyavuni. Kiungo wa zamani wa Yanga, Salum Telele, nusura aipatie Ndanda bao la kuongoza dakika ya 35 baada ya kuambaa na mpira hadi katika eneo la hatari, lakini hesabu zake ziligonga mwamba baada ya kipa Deogratius Munishi kuuwahi mpira na kuokoa hatari hiyo. Kipindi cha pili kilianza kwa Ndanda kufanya shambulizi la kushtukiza dakika ya 58 kupitia kwa Right Hamis, lakini shuti alilopiga lilidakwa na kipa wa Yanga. Yanga walifanikiwa kuongeza karamu ya mabao baada ya mlinzi, Vicent Bossou, kufunga bao la nne katika dakika ya 89 akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Juma Abdul. Mchezo mwingine wa ligi hiyo ulichezwa katika Uwanja wa Manungu, Morogoro ambapo wenyeji Mtibwa Sugar waliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Majimaji FC ya Songea. Matokeo hayo yameiwezesha Mtibwa kupanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi baada ya kufikisha pointi 30 na kuishusha Kagera Sugar yenye pointi 28 hadi nafasi ya nne.
4
Habari kutoka kambi ya mazoezi ya Harambee Stars nchini Misri zinadai kuwa beki wa kati ambae ni tegemezi Josh Onyango hatocheza mechi ya ufunguzi dhidi ya Algeria leo. Mlinzi huyo wa club ya Gor Mahia anaugulia maumivu ya kifundo cha mguu  aliyopata wakati wa mazoezi. Na bado haijwekwa wazi ni mechi gani mchezaji huyo atazikosa, mechi inayofuata ambayo itakua siku ya Alhamis ni muhimu kwani watakua wanakipiga na Tanzania. Kukosekana kwa Onyango, Itabidi Sebastian Migne  amnyanyue benchi David Owino ili aweze kushirikiana na Musa Mohamed ambae amecheza mechi zote za kufuzu. Machaguo mengine ni Joseph Okumu ama Bernard Ochieng anayekipiga katika klabu ya Vihiga United. Onyango mwenye umri wa miaka 27 ukiachana na mziki wake uwanjani akiwa na Harambee Stars, amekua maarufu sana mitandaoni siku za karibuni kutokana na staili yake ya ndevu alizoaamua kuzipaka rangi na kuonekana kama mzee. Kila la kheri majirani! Come on Stars! #matchday The 15 years wait is over. Leo ni leo🇰🇪🇰🇪#Tunaweza #AFCON2019 #Harambeestars #BetinNaStars A post shared by Kenya National Team. (@harambee_stars) on Jun 22, 2019 at 10:15pm PDT    
4
Derick Milton, Meatu Bodi ya pamba nchini imewatoa hofu wakulima wa zao hilo wilayani Meatu mkoani Simiyu, kuhusu upatikanaji wa mbegu za zao hilo katika kuelekea msimu mpya wa kilimo ambao tayari umeanza. Akiongea na wakulima wa pamba katika vijiji vya Isengwa na Mwandoya wilayani humo, pamoja na kamati ya mazao ya Wilaya Mkaguzi wa pamba kutoka Bodi hiyo Wilaya Jeremiah Kalissa amesema mbegu zipo za kutosha. Kalissa amesema jumla ya kampuni sita za pamba zimepewa kazi ya kusambaza mbegu kwa wakulima, ambapo kati ya tani 2,290 zinazohitajika kwenye wilaya hiyo tani 1,850 tayari zimesambazwa kwa wakulima. “Mbegu zipo za kutosha hakuna mkulima atakayekosa mbegu msimu huu, tumeanza kusambaza kwa haraka… hivyo niwatoe hofu juu ya hilo, pia viuatilifu navyo vitakuja kwa wakati,” amesema Kalissa. Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo Dk. Joseph Chilongani ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya mazao, amewataka wakulima kuwa wakweli katika kuchukua mbegu hizo kulingana na maeneo yao ya kilimo. “Ukibainika unafanya hivyo tutachukulia hatua kali, baadhi yenu msimu uliopita walifanya hivyo, serikali imetoa fursa kwa kila mkulima hata kama huna fedha za kununulia utapewa lakini unakopeshwa siyo bure,” amesema Dk. Chilongani.
3
NYOTA ya uwekezaji katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), imeendelea kung’aa na itazidi kung’aa mwaka 2019.Ripoti ya Benki ya Biashara ya Rand (RMB) ya Afrika Kusini, imeonesha kuwa Afrika Mashariki itakuwa kitovu cha uwekezaji barani Afrika mwaka huu. Hii ni kutokana na juhudi za nchi wanachama wa jumuiya hiyo kuboresha miundombinu mbalimbali ikiwemo barabara, reli hasa ya SGR, umeme, usafiri wa anga na uchimbaji wa mafuta na gesi, ambavyo ni vivutio vya uwekezaji duniani.Utafiti huo uliopewa jina la ‘Wapi Pa Kuwekeza Barani Afrika 2019’ ulihusisha kanda tano za bara la Afrika, za Kaskazini, Magharibi, Kati, Mashariki na Kusini, ukiangalia juhudi na mipango endelevu ya kuimarisha uwekezaji kikanda. Kwa mujibu wa utafiti huo, tangu mwaka 2017 hadi mwaka huu bara la Afrika limepiga hatua kutokana na shughuli mbalimbali zinazofanywa na baadhi ya mataifa, ambazo zimesababisha kusiwe na ugumu katika upatikanaji wa fedha.Baadhi ya shughuli hizo ni vita dhidi ya rushwa, kuimarishwa kwa miundombinu yenye kuwasaidia wananchi katika kupata huduma mbalimbali na utawala bora. Kwa kuangalia nchi moja moja katika jumuiya hiyo, ripoti hiyo imeonesha kuwa Kenya imeongoza kwa nchi za kanda hiyo, kuvutia uwekezaji kuliko mataifa mengine. Sababu iliyotolewa ambayo iliisaidia Kenya kuwa kivutio kikubwa cha uwekezaji ni kufanyika kwa maridhiano ya kisiasa kati ya Rais Uhuru Kenyatta na Kiongozi Mkuu wa Upinzani, Raila Odinga yaliyofikiwa mwezi Machi mwaka jana.Hali hiyo inatajwa kuleta mazingira bora ya kuvutia wageni wakiwemo watalii na wawekezaji katika sekta mbalimbali. Ripoti hiyo ilisema sehemu yenye msuguano wa kisiasa, baina ya watu wake, haivutii wawekezaji, badala yake inawafukuza. Nafasi ya pili ya kuwa na mazingira bora ya kuvutia uwekezaji, kwa mujibu wa ripoti ya utafiti huo, imechukuliwa na Rwanda.Taifa hilo limetajwa kuwa lenye uchumi unaokua kwa haraka na limeongeza mara mbili ya mazingira ya ukuaji wa uchumi wake katika kipindi cha miaka kumi. Kitu kingine kilichoifanya Rwanda kupata mafanikio hayo ni juhudi za serikali katika kuwekeza katika ukuaji wa viwanda, vinavyomilikiwa na wazawa na maendeleo ya teknolojia. Nafasi ya tatu imechukuliwa na Tanzania, kwa kuwa na mazingira rafiki ya uwekezaji wa ndani na kimataifa. Mambo yaliyotajwa katika ripoti hiyo yaliyoiinua Tanzania ni usimamizi mzuri wa kodi kwa wawekezaji.Vilevile Tanzania imesifiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na juhudi zake za kuanzisha kanda maalum za uwekezaji. Hali hiyo inatajwa kuwa inawasaidia wawekezaji kuwa na uhakika wa uwekezaji wa fedha zao. Pia, juhudi za serikali za kuwekeza katika miundombinu hasa ya barabara, miundombinu ya reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam kupitia Morogoro na Dodoma.Lengo la Serikali ya Awamu ya Tano ni kuunganisha reli hiyo hadi Mwanza, hali itakayorahisisha usafiri na usafirishaji kutoka na kwenda Kanda ya Ziwa. Tanzania imetajwa pia katika uwekezaji katika nishati ya umeme na gesi, kiasi cha kuwa kimbilio kwa wawekezaji wa kimataifa. Hii inashajihishwa na uwepo wa usafiri wa uhakika wa ndege, baada ya kufufuliwa kwa Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL), ambayo mpaka sasa ina ndege saba.Nchi za Sudan Kusini na Burundi, zimetajwa kuwa ni zenye changamoto ya kiuwekezaji, lakini bado zinapewa nafasi kubwa ya kuwa vivutio vya uwekezaji kutokana na matukio ya kisiasa ya hivi karibuni. Kwa upande wa Sudan Kusini, muafaka wa kisiasa uliofikiwa baina ya serikali na wapinzani, umetoa uhakika wa kuwa na amani katika siku zijazo.
3
TIMU ya taifa ya soka ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, jana ilipoteza mchezo wa nusu fainali wa Michuano ya Kombe la Chalenji dhidi ya Uganda kwa bao 1-0 na sasa itacheza kuwania nafasi ya tatu dhidi ya Kenya kesho.Michuano hiyo inayoshirikisha timu za nchi za Afrika Mashariki na Kati chini ya Cecafa, inafanyika mjini Kampala, Uganda. Katika mchezo huo uliokuwa mkali na wenye kusisimua, bao pekee la Uganda lilifungwa na Fahad Bayo dakika ya 86.Wenyeji hao walicheza mpira kwa kasi kipindi cha kwanza na kutengeneza nafasi zaidi ya mbili lakini kipa Aishi Manula alikuwa makini na kuzicheza. Manula hakudumu katika mchezo baada ya dakika ya 37 kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Metacha Mnata aliyedumu hadi kumalizika kwa mpira.Aidha, kwa upande Kili Stars, pia walitengeneza nafasi zaidi ya moja kipindi cha kwanza ila kipa wa Uganda alikuwa makini kwa kupangua moja ya shuti kali la Eliuta Mpepo. Kipindi cha pili timu zilianza kushambuliana kwa zamu na kuendelea kutengeneza nafasi kwa vipindi tofauti lakini hawakuzitumia ipasavyo zaidi ya Uganda iliyochomoza kwa ushindi uliodumu hadi kumalizika kwa mpira.Baada ya Uganda kuongoza, Kocha Mkuu wa Kili Stars, Juma Mgunda alifanya mabadiliko kwa kuwatoa Dickson Kibabage na Eliuta Mpepo na kuingia Cleofas Mkandala na Paul Ngonga lakini mabadiliko hayo hayakusaidia lolote kwani muda ulikuwa umeshakwenda.Mchezo mwingine uliochezwa jana Kenya ilipigwa mabao 4-1 dhidi ya Eritrea. Kwa maana hiyo, fainali itakuwa ni Uganda dhidi ya Eritrea huku nafasi ya tatu Kili Stars ikitarajiwa kuchuana na Kenya.Kili Stars na Kenya zilipangwa kundi moja B, na katika mechi yao Kenya ilishinda bao 1-0, matokeo yanayoifanya Kili ijipange kisawasawa kwani ni mechi ambayo haitakuwa rahisi.
4
['Mkenya Eliud Kipchoge ameweka jina lake katika vitabu vya historia , akimaliza kilomita 42 za mbio za marathon kwa saa moja dakika 59 na sekunde 40 katika shindano la Ineos siku ya Jumamosi nchini Austria Vienna. ', 'Hatahivyo muda huo bora uliowekwa na bingwa huyo hautatambulika kama rekodi ya dunia.', 'Kulingana Shirika la Riadha duniani IAAF , kwa mbio yoyote kufikia sheria zake na hivyobasi kutambulika kama rekodi ya dunia kuna masharti yanayopaswa kufuatwa kulingana na chombo cha habari cha AFP.', 'Wakati wa jaribio la kwanza la mbio hizo za marathoni huko Monza nchini Itali miaka miwili iliopita, Kipchoge alipatiwa vinywaji huku wadhibiti mbio hizo wakibadilishwa mara kwa mara, hatua iliokiuka masharti ya IAAF. ', 'Siku ya Jumamosi , alipewa vinywaji kila baada ya kilomita 5 na hivyobasi kukiuka sheria hizo za shirikisho la riadha duniani. ', 'Mkimbiaji huyo mwenye umri wa miaka 34 tayari anashikilia rekodi ya dunia miongoni mwa wanaume katika umbali huo akiwa na muda wa saa mbili dakika moja na sekunde 39, ambao aliweka katika mbio za Berlin tarehe 16 mwezi Septemba 2018. ', 'Kulingana na AFP , barabara hiyo ilikuwa imeandaliwa hali ya kwamba ingemchukua Kipchoge sekunde 4.5 zaidi kulingana na uchanganuzi wa wataalam wa michezo katika chuo kikuu cha Vienna. ', 'Kwa jumla aliweza kushuka mita 26 na kupanda mita 12 , walisema wataalam hao. ', 'Mbio hizo za marathon zimekuwa na ushindani mkali katika kipindi cha miaka 16 iliopita kati ya wanariadha wa Kenya na wenzao wa Ethiopia. ', 'Mataifa hayo mawili ni washindani wakuu wa mbio ndefu uwanjani. ', 'Rekodi ya Kipchoge ilikaribia kuvunjwa na raia Muethiopia Kenenisa Bekele ambaye alikimbia saa 2 dakika moja na sekunde 41 ikiwa ni sekunde mbili pekee kabla ya kuivunja rekodi hiyo. ', 'Mbio hizo za Viena hazikuwa mashindano bali zililenga kuwapa motisha mamilioni ya watu duniani. Na Kipchoge amefanikiwa. ', 'Katika mahaojiano na vyombo vya habari , Kipchoge alisema kwamba mbio hizo za Vienna zililenga kuwapatia changamoto wanadamu katika maisha yao ya kila siku. ', 'Pia aliwashutumu wakosoaji wake. ', "Ninakimbia kuweka historia , ili kuuza #NoHumanLimited na kuwapa motosha zaidi ya watu bilioni 3 . Sio swala la fedha bali kubadilisha maisha ya watu'', alinukuliwa akisema."]
4
Msanii wa Bongo fleva Ommy Dimpoz amemkataa Mwana FA ambaye jana alitangazwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona na sasa yupo karantini akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya. Dimpoz alionyesha kumkataa Mwana FA kupitia video aliyopost katika ukurasa wake wa instagramu ambapo mtu alimpiga simu kuumuuliza iwapo amekutana na msanii huyo hivi karibuni lakini alimkwepa akisema hana ukaribu naye siku hizi. Katika video hiyo ambayo pengine ni ya kuigiza Ommy alisema Mwana FA marafiki zake ni waimbaji wa Hip Hop, tajiri wa GSM na Alberto Msando. Hata hivyo kuonyesha kuwa yalikuwa ni masilahala maelezo ya video hiyo ya Ommy ilikuwa ikiwashauri watu kutowakimbia waathirika na badala yake kupima. “Dawa sio kuwakataa marafiki zetu kisa Wamekutwa na Maambukizi,Dawa ni kwenda kupima kama ukijiona una Dalili Zilizotajwa za Corona” Dawa sio kuwakataa marafiki zetu kisa Wamekutwa na Maambukizi,Dawa ni kwenda kupima kama ukijiona una Dalili Zilizotajwa za Corona #StaySafe #StayHome #WashHands A post shared by Ommy Dimpoz (@ommydimpoz) on Mar 20, 2020 at 5:24am PDT  
1
FRANCIS  GODWIN, IRINGA WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya  Waziri Mkuu (Sera  ,Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu  wenye  Ulemavu, Jenista Mhagama  ameagiza  ujenzi  wa  vituo  20 vitakavyotoa  huduma  za ugonjwa   Ukimwi kwa   wasafiri wa  masafa marefu vinavyojengwa chini ya Programu  ya Sattf   barabara kuu ya Dar es Salaam  kwenda nchi za  kusini mwa Tanzania kukamilisha ujenzi  huo ndani ya  mwezi mmoja. Alitoa  agizo  hilo juzi,baada ya kuwekaji wa jiwe la msingi  kituo cha afya  Ipogolo  mjini  Iringa  kwa niaba ya  vituo  vingine. Alisema hajafurahishwa na kasi  ndogo ya  ujenzi wa vituo  hivyo  ambavyo  kimsingi ujenzi  wake  ulipaswa  kukamilika tangu  Oktoba, mwaka huu. Alisema  ujenzi  wa  vituo   20  kutoka  Dar es Salaam  hadi  Tunduma – Momba mpakani  wa Tanzania na  Zambia,Serikali  imekwishatumia  Dola za  Marekani milioni 3,  japo  kasi ya ujenzi  inasuasua. Alisema  kutokana na  kasi ya Serikali uboreshaji wa  huduma  za  afya   ujenzi wa vituo  hivyo  utasaidia   kupunguza kasi ya maambukii ya  virusi vya ugonjwa huo kwa  wasafiri   wanaotumia barabara  hizo. Alisema kupitia   fedha  hizo pamoja na kukamilisha ujenzi  wa vituo, pia  zitawezesha  kununua vifaa vya  kisasa na kuweka mazingira  wezeshi ya  kufundisha  wataalamu 10 kila  kituo watapata mafunzo. Alisema lengo la kuwafundisha  wataalamu hao,  ni  kuondoa  usumbufu  wa  uhaba wa wahudumu katika vituo ili  wateja  watakapofika wapate huduma kwa wakati. Alimtaka   Mkurugenzi  Mkuu wa  Tume ya Kuthibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS )  kuangalia  uwezekano wa kuanzisha mpango wa ujenzi wa  vituo kama  hivyo maeneo ya mipakani. Alisema  ili  vituo  lazima  viweze endelevu na  kutoa  huduma  zake  kwa kipindi  kirefu zaidi ni  vizuri suala la  utunzaji  na usimamiazi wa miundombinu. Katika  hatua  nyingine,Waziri Mhagama  aliahidi  kuanzisha  ujenzi  wa chumba  cha upasuaji na chumba  cha uzazi  kituo cha afya Ipogolo  na yeye atachangia  mifuko 100 ya saruji na bati 100 kama  sehemu ya  kuunga mkono. ” Ninalazimika  kuchangia bati  na saruji  ili  kuanza  ujenzi  wa  chumba cha upasuaji na chumba  cha uzazi,  nimefurahi  kukutana na Rosemary  Mwenda  ambae  leo amepata mtoto  katika  kituo hiki tena mtoto wa  kike  ambae  nimempa jina la Jenista,mimi ni mama  yake wa hiari baada ya mzazi wake  kufikisha ombi la kujengewa  vyumba,”alisema. Kuhusu    kasi ya mambukizi ya virusi wa  vya  Ukimwi (VVU) mikoa ya  Njombe , Iringa na Mbeya, Mhagama  alisema   inatisha  na kuna haja ya  mikoa hiyo  kuweka mkakati wa  kupunguza kasi hiyo. Mkuu wa  Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema  mkoa huo umepatiwa  vituo vinne   Wilaya ya Kilolo,kimoja  na  Iringa  vituo  vitatu ambavyo  vitasaidia  kupunguza kasi ya maambukizi. Mkurugenzi  Mtendaji wa TACAIDS,Dk. Leonard Maboko  alisema  Tanzania ni miongoni mwa  nchi  za   kusini  mwa Jangwa la  Sahara  ambazo zinakabiliwa na kiwango kikubwa  na tatizo la ugonjwa huo,huku takwimu  zikionyesha  watu takribani milioni 37.9 wanaishi na maambukizi ya  VVU mwishoni  mwaka 2018 duniani , kati ya hao asilimia   53 wapo nchi  za  mashariki na kusini  mwa Afrika .
3
Na Lilian Justice, KIJIJI cha Kisimaguru  wilayani Mvomero katika Kata ya Hembeti kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa zahanati, imefahamika Hali hiyo husababisha wagonjwa kubebwa kwa machela zaidi ya kilomita 20 milimani kusaka huduma ya afya katika zahanati ya Hembeti. Hayo yalielezwa jana na Diwani wa Kata ya Hembeti, Peter Mdidi katika mahojiano maalumu na Mtanzania. Mdidi alisema wajawazito wanaotakiwa kujifungua hubebwa na machela na hivyo wengine kujikuta wakijifungulia njiani. "Kutokana na changamoto ya umbali mrefu wa kufika katika zahanati ya Hembeti kunasababisha wajawazito kujifungulia njiani"alisema Mdidi. Alisema kijiji kimeshajiwekea mkakati wa kujenga zahanati yake na hivi sasa wananchi wameanza kuchangia nguvu kazi. Diwani huyo aliwaomba wadau na serikali wilayani humo kuchangia ujenzi huo uweze kukamilika kwa wakati. "Tayari wananchi wameonyesha moyo wa kuchangia nguvu kazi katika ujenzi  huo hivyo tunawaomba wadau watuunge mkono kuwaondolea adha wananchi," alisema Mdidi. Alisema Kijiji cha Kisimaguru kina jumla ya wakazi 800 aliwaomba wadau kutoingiza masuala ya siasa na badala yake waunge mkono juhudi hizo.
3
Na VERONICA ROMWALD- DAR ES SALAAM KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii, imeshangazwa na kitendo cha serikali kutozipatia fedha za miradi ya maendeleo Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) kama walivyoomba na kuidhinishwa na Bunge. Katika mwaka wa fedha 2016/17, Muhimbili iliomba kiasi cha Sh bilioni 4 na MOI iliomba kupatiwa Sh bilioni 4.8, lakini fedha hizo hawajapatiwa hadi hivi sasa. Yalibainika hayo jana wakati kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Peter Serukamba ilipofanya ziara katika hospitali hizo. Kutokana na hali hiyo, wajumbe walimbana kwa maswali Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangwalla wakimtaka aeleze sababu za Serikali kutotoa fedha hizo. Hoja hiyo iliibuka baada ya Mkurugenzi wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru kueleza kwamba hawajapokea fedha hizo walizoomba. “Tuliomba Sh bilioni 4, hatukupewa fedha yoyote, katika kipindi cha Julai hadi Desemba, 2016 tulipokea misaada ya thamani ya Sh milioni 218.044 kutoka kwa wahisani, na tulipokea mkopo wa Sh bilioni 7.897 kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),” alisema. Alisema fedha hizo walizitumia kununua vifaa tiba ikiwamo Ct-Scan na ukarabati wa wodi na vyumba vya upasuaji. Profesa Museru alisema kwa kuwa hospitali hiyo ina muda mrefu tangu imejengwa, inahitaji ukarabati mkubwa na ununuzi wa vifaa tiba kwani vilivyopo vimechakaa na vingi vimeharibika. Akichangia hoja hiyo, Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), alisema jambo hilo linashangaza kwani wabunge wanapopitisha bajeti, Serikali inakuwa imeelezwa nini cha kufanya. “Kila mwaka tunapitisha bajeti, lakini kila tunapopita tunaambiwa fedha za maendeleo hazijapelekwa, kwanini hazipelekwi wakati zilipitishwa?” alihoji. Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (Chadema), alisema ni muhimu Serikali ikawa makini katika suala hilo na kwamba bajeti inapopitishwa ipelekwe kwa wakati. Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndungulile (CCM), alisema Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kutengeneza vifaa tiba, hivyo wakati umefika ikashirikiana na watu wengine kwa kuwaruhusu kuwekeza vifaa tiba na hospitali zake zibaki kutoa tiba. Akijibu hoja hizo, Dk. Kigwangwalla alikiri kuwapo changamoto ya fedha inayozikabili hospitali hizo, hata hivyo alisema zinafanyiwa kazi na Serikali.
3
Na Mwandishi Wetu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesema umepania kukifufua na kukiendeleza Chuo cha Siasa , Uongozi na Ujasiriamali kilichopo Ihemi mkoani Iringa. Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM,  Shaka Hamdu Shaka amesema    lengo ni kuwapika , kuwafundisha na kuwaandaa katika saikolojoa vijana ili kuwapa stadi za maisha na kujitegemea katika uchumi. Alikuwa akizundua mafunzo elekezi ya ujasiriamali na uhamasishaji   kwa kuzitambua fursa za kujiajiri kwa  vijana wa  Wilaya ya Ubungo katika ukumbi wa Texas Manzese,   Dar es Salaam. Shaka alisema hakuna taifa lolote duniani lenye uwezo wa kuwapatia ajira vijana wote. Alisema  badala yake vijana huwezeshwa katika elimu kwa kufundishwa stadi za maisha, ufanyaji bora wa biashara, uendeshaji miradi , kutambua na kuzingatia vyema miiko ya chama, siasa yake na itikadi. Alisema njia pekee ya kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli na kuinua maisha ya vijana dhidi ya umasikini na matumizi bora ya maliaasili na rasilimali za taifa ni vijana wenyewe kujitambua, kujituma na kujitegemea. “Ili vijana waendesha miradi yao ya uchumi na kuwapa manufaa, biashara na kujitegemea wanahitaji kujengwa uwezo, kupewa mbinu za kisasa na kufundishwa stadi za maisha kwa weledi na umakini,”alisema Shaka. Alisema chuo hicho sasa licha ya kutumika kuwafundisha ujasiriamali vile vile kitafundisha siasa ya chama, itikadi, na uzalendo ikiwamo kuwaeleimisha katika masuala ya kujitegemea na ufundi. Akizumgumzia maendeleo ya uchaguzi ndani ya chama na jumuiya zake,   aliwataka watendaji wa jumuia kusimaia miongozo na kanuni huku wagombea wakitakiwa kutojihusisha na vitendo vya rushwa. Alisema uchaguzi ni lazima utoe viongozi wenye uthubutu, uwezo wa kuitetea jumuiya, kuipigania na kuweka katika taaswira ya kuheshimika jambo litakalosaidia kuwapata viongozi  bora, makini, wenye ujasiri na uzalendo. “Nasema tena hakuna mgombea atakayepitishwa na vikao vyetu ikiwa sifa zake zina kasoro, upungufu au zwa kuokotezaokoteza. “Tutampekua kila mgombea na tukimuona hatokani na CCM tutamtosa bila ya kuutazama uso wake,” alisistiza.
3
Mwandishi Wetu -Singida BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 katika wilaya kadhaa nchini. Misaada iliyotolewa na benki hiyo inayoongoza kwa kutengeneza faida kati ya benki zote zinazofanya biashara humu nchini ndani ya miezi mitano mwaka huu, inahusisha vifaa vya ujenzi, madawati na vifaa vingine vinavyowezesha ukamilishaji wa miradi ya afya,elimu na usalama wa raia. Benki  ya NMB imeshatoa  msaada wa  vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa mikoa ya Kanda ya Kati. Akifafanua kuhusu misaada hiyo wakati akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani ingida, Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi, alibainisha kuwa misaada hiyo ya zaidi ya Sh milioni 200 iliyotolewa imelenga sekta ya elimu, afya  na majanga kwa mikoa mitatu ya  Kanda ya kati. Akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, MkoaniSingida, katika shule ya Sekondari ya New Kiomboi, Mlozi alisema fedha hizo zilizotolewa na NMB zimetumika kununua madawati, viti vya shule za sekondari,vitanda na vifaa tiba kwenye sekta ya afya. Aidha, alisema lengo la misaada hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali. Pia alisema misaada hiyo imekabidhiwa kwa baadhi ya shule, zahanati, hospitali katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Pia NMB walikabidhi madawati 250 na vitanda 80 vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 29.5 kwa baadhi ya shule za Wilaya ya Iramba mkoani humo. Katika hatua nyingine, Benki hiyo imevipatia kituo cha Polisi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro pamoja na shule ya msingi Msowelo mabati 160 yenye thamani ya Sh5 milioni kwa ajili ya kuezekea maboma. NMB iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni mpango wa kuzipunguza baadhi ya changamoto kwa taasisi za serikali hapa nchini, Meneja wa NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus, alisema na kubainisha kuwa msaada huo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ili kusaidia kuinua miradi ya maendeleo. Baraka alisema kuwa kati ya mabati hayo, kituo cha polisi wilaya kimepa tamabati 80 huku shule ya msingi Msowelo nayo ikipata mabati 80.
5
Na AVELINE KITOMARY TAASISI ya Mifupa Muhimbili (MOI) imewahimiza watu mbalimbali, kampuni na taasisi kujitokeza kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa wa dharura wanaofikishwa katika taasisi hiyo. Akizungumza jana na MTANZANIA Jumapili, Ofisa Habari wa taasisi hiyo, Patrick Mvungi, alisema tangu kuingia kwa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (Covid-19), idadi ya watu wanaochangia damu imepungua hali inayosababisha wagonjwa kukosa damu. Alisema asilimia 90 ya wagonjwa waliopo katika taasisi hiyo hufanyiwa upasuaji, hivyo uhitaji wa damu ni mkubwa kwa sasa.  “Utaratibu ni kwamba kama ndugu yako anaumwa unakuja kutoa damu ili aweze kufanyiwa upasuaji na mgonjwa kuongezewa damu, huu bado upo na hatujaufuta. “Hapa tunaomba kupata damu kwa ajili ya wale wagonjwa wa dharura, mfano mtu kapata ajali, hapo mnampokea utakuta ameishiwa damu na anahitajika kuongezewa, lakini kwa wakati huo ndugu zake bado hawajui hata kama yuko hospitali, hawa ndio wanaohitaji msaada zaidi,” alisema Mvungi. Alisema wameweka utaratibu maalumu ambao utasaidia wachangiaji kuepuka misongamano na kwamba taratibu zote za kujikinga zitafuatwa. “Watu wajitokeze hata kama ni vikundi, tutaweka utaratibu maalumu ambao hautasababisha msongamano kwani watakuja kidogo kidogo, hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Mvungi. Alisema kuwa damu ni kitu pekee ambacho hakiwezi kununuliwa, hivyo amewataka wananchi walichukulie uzito suala hilo. Aliwataka Watanzania kuwa na moyo wa upendo kwa kuokoa maisha ya wenzao kwa kuchangia damu, hasa majeruhi wa ajali ambao hufikishwa kwa dharura katika taasisi hiyo.
0
TAMASHA maalumu la kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, linatarajiwa kufanyika Oktoba 13 mwaka huu katika kijiji cha Butiama, Mara na kuhudhuriwa na watu zaidi ya 1,000 kutoka mikoa mbalimbali. Kwa mujibu wa waandaaji wa tamasha hilo, Kampuni ya Miranda, linatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Spika wa Bunge mstaafu Pius Msekwa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka na baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Mkurugenzi wa Kituo cha Kuhifadhi Utamaduni wa Wazanaki (KIHUZA) Mashaka Mgeta, alisema lengo la tamasha hilo litakalohusisha michezo mbalimbali ikiwemo riadha, ni kumuenzi kiongozi huyo ambaye ni muasisi wa Taifa, aliyefariki miaka 19 iliyopita na kuzikwa kijijini humo. “Tumeamua kuandaa tamasha hili kutokana na msukumo uliotolewa hivi karibuni na Rais John Magufuli alipotembelea Mara na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa kutokana na mambo mengi na makubwa aliyolifanyia Taifa hili enzi za uhai wake ikiwa ni pamoja na kutuletea uhuru,” alisema Mgeta. Kwa upande wake mratibu wa tamasha hilo Kulwa Karedia, alisema kuanzishwa kwa tamasha kumelenga pia kuendelea kulitangaza jina la muasisi huyo wa Taifa ili kuenzi yale mambo yote mazuri aliyoyafanya, ikiwemo kusaidia kupatikana kwa uhuru kwa mataifa mengi hasa yaliyopo kusini mwa Afrika.Alisema kupitia tamasha hilo, wanaamini watu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi watakaoshiriki watapata fursa ya kufahamu mambo mengi kuhusu kiongozi huyo, pamoja na utamaduni wa kabila lake la Wazanaki na hata namna alivyoishi vizuri na watu mbalimbali wakiwemo kutoka jamii yake. Karedia alisema tamasha hilo mbali na washiriki kushindana katika mchezo wa kuendesha baiskeli, pia kutakuwa na matembezi maalumu katika barabara iliyokuwa ikitumiwa na kiongozi huyo, pamoja na riadha kwa makundi mbalimbali.Kwa upande huo wa riadha, alisema kutakuwa na mbio za kilomita 10, zitakazowashirikisha wananchi wa wilaya zote za Mara, kilomita 5 kwa wageni waalikwa na kilomita 2 kwa watoto wadogo, lengo ni kushirikisha makundi ya aina yote.
4
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda aliyasema hayo jana bungeni wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2015/16.Dk Kigoda alisema ujenzi wa kiwanda hicho eneo la Tamco wilayani Kibaha, umekamilika na kwamba Rais Kikwete anatarajiwa kuwa atakizindua.Alisema teknolojia itakayotumika kuzalisha viuadudu ni ya kipekee barani Afrika na hivyo viuadudu ni ya kipekee vitakavyozalishwa vitasaidia kuua mbu na kutokomeza ugonjwa wa malaria nchini na pia vitauzwa nje.Alisema vitaliingizia Taifa fedha za kigeni takriban dola za Marekani milioni 48.6 kwa mwaka na ajira zipatazo 670.“Kukamilika kwa mradi huo kunatimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ilipoingia madarakani kuwa itachukua hatua madhubuti za kutokomeza malaria,” alisema.Kuhusu mradi wa magadi soda huko Engaruka mkoani Arusha, alisema Wizara kupitia Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), ilikamilisha uainishaji wa eneo la kilometa za mraba 410 katika Bonde la Engaruka wilayani Monduli linalohitajika katika ujenzi wa kiwanda na miundombinu yake, makazi ya wafanyakazi na viwanda vingine vya kuongeza thamani vinavyotumia magadi soda kama malighafi.Alisema hivi sasa Wizara kupitia NDC iko katika hatua za mwisho za kumpata mbia atakayeshirikiana na NDC katika kujenga kiwanda hicho.“Ujenzi wa kiwanda cha magadi huko Engaruka utaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazozalisha kwa wingi magadi hayo duniani ikizidiwa na Marekani pekee,” alieleza Dk Kigoda.
5
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemwagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo kusimamia ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu ya Chuo cha Ualimu Mpuguso mkoani Mbeya ili majengo hayo yaweze kutumiwa na walimu tarajali.Ametoa agizo hilo kutokana na kusuasua kwa ujenzi wa miundombinu yake unaotekelezwa na mkandarasi, kampuni ya Lukolo Construction.Baada ya ukaguzi, Profesa Ndalichako alibaini mradi huo ukitekelezwa kwa hali isiyoridhisha baadhi ya maeneo yakiwa chini ya kiwango.Alisema pamoja na mkandarasi kuongezewa muda, ameshindwa kukamilisha kazi kwa wakati jambo lililofanya chuo kisitumie miundombinu na serikali kuchelewa kufikia malengo ya uboreshaji na upanuzi chuo hicho.“Naelekeza mradi huu ukamilike Desemba 30 tena kwa ubora kama ilivyopangwa.Katibu Mkuu afuatilie na mkandarasi akishindwa kukamilisha mchukulieni hatua,” alisema Waziri alisema, makubaliano mapya baada ya kurudishwa kazini ni kazi kukamilika Desemba 30, 2019 lakini hadi sasa mkandarasi haonekani eneo la mradi na hakuna kinachoendelea hapo.Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alimweleza waziri mkandarasi asipokamilisha kazi hiyo kwa muda uliopangwa atachukuliwa hatua na mkoa utafuatilia utekelezaji wake
3
NA MWANDISHI WETU WASANII nguli wa muziki nchini, Ben Pol, Ali Kiba, Fid Q na Vanessa Mdee, wataungana na wasanii wengine 27 barani Afrika katika msimu wa tatu wa maonyesho ya  burudani ya muziki, maarufu kama Coke Studio Africa litakaloanza mapema wiki ijayo. Onyesho la mwaka huu ni tofauti na yaliyopita kwa kuwa litaendana na mabadiliko yaliyopo katika muziki duniani ‘Kolabo’. Kolabo ya wasanii 55 itashirikisha wasanii wawili kutoka nchi mbili tofauti kuimba nyimbo mbili za mitindo tofauti. Mtindo wa Kolabo uliwahi kutumika hapo awali katika maonyesho ya televisheni, sinema na wakati wa kupiga muziki mchanganyiko ambapo safari hii utawawezesha wasanii husika kuwa wabunifu na kuboresha viwango vyao vya sauti za uimbaji. Wasanii wengine watakaokuwa kwenye onyesho hilo litakaloanza kuonekana kwenye luninga Oktoba 10, mwaka huu ni Wangechi na Victoria Kimani wa Kenya, Maurice Kirya (Uganda), mwanamuziki nguli kutoka Nigeria, 2Face. Kwa mujibu wa waandaaji, onyesho kwanza litarushwa kupitia kituo cha televisheni cha Clouds Oktoba 10 kuanzia saa 12 jioni.  
1
WATUMISHI wa serikali walioshindwa kukamilisha malipo ya nyumba za serikali walizouziwa mwaka 2002, wapo hatarini kunyang’anywa nyumba hizo. Mwaka 2002 Serikali ya Awamu ya Tatu ilitangaza kuuza nyumba zake kwa watumishi wa umma sehemu mbalimbali nchini, ambako ilitoa muda wa miaka 10 wawe wameshakamilisha malipo hayo huku wakizuiliwa kubadilisha matumizi hadi miaka 25 ipite.Hivyo muda wa kuwa wamemaliza kulipa fedha hizo umeshapita, ambao ni mwaka 2012 huku ule wa kuanza kubadilisha matumizi ni mwaka 2027. Lakini, hata hivyo, gazeti hili limebaini kuwa baadhi ya waliokuwa watumishi wa umma na wengine bado wanaendelea na utumishi wa umma, waliouziwa nyumba hizo, hawajamalizia kulipa fedha na wamekiuka mkataba wa mauziano kwa kubadilisha matumizi ya nyumba hizo.Wapo ambao miaka 10 imepita hawajamaliza kulipa gharama na wameshabadilisha matumizi ya nyumba hizo, kwa kujenga nyumba za kisasa za kupangisha (apartments), kuingia ubia na kujenga maduka makubwa, ofisi na hata baa au kumbi za burudani na wengine wameziuza.Hayo yamefanyika hasa kwenye maeneo waliyokuwa wakiishi watumishi wa ngazi za juu serikalini kama vile Oysterbay, Masaki, Upanga na Mikocheni, Dar es Salaam. Katika kupata uhalisia wa ni idadi ya nyumba ngapi za aina hiyo, ambazo hazijamaliziwa kulipiwa gharama zake na kiasi gani cha fedha, ambazo serikali ingetakiwa kupata kama zingelipwa kwa wakati, gazeti hili lilifanya mahojiano maalumu na Kaimu Meneja wa Sehemu ya Miliki na Huduma za Nyumba wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Erasmi Tarimo.Mahojiano hayo yaliyochukua takribani dakika 45 yalifanyika kwenye ofisi ya Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Daudi Kondoro, ambaye pia alikuwa akifuatilia majibu ya kina kutoka kwa Tarimo.Tarimo alifafanua kuwa kwa waliomaliza kulipia gharama zote za nyumba, hawakupewa kibali na TBA cha kubadilisha matumizi, kwa kuwa wakishamaliza kulipa gharama, nyumba zinakuwa mali zao, ila sasa kama wakipewa kibali na halmashauri za manispaa waliopo, hilo linakuwa sio tena suala la TBA.Alisema kwa waliobadilisha matumizi huku wakiwa hawamaliza hata kulipa fedha za serikali, TBA ina uwezo wa kuwanyang’anya. Kuhusu idadi kamili za wadaiwa hao na fedha wanazodaiwa kwa ujumla, gazeti hili linaendelea kusubiri takwimu halisi kutokea TBA, ambapo Kondoro licha ya kuagizwa kutolewa kwa takwimu hizo, agizo lililotekelezwa na Tarimo kwa muda wa siku saba sasa gazeti hili linangojea taarifa rasmi kutoka TBA.Hiyo ni kutokana gazeti hili kutakiwa kuwasilisha barua rasmi ya kuomba takwimu hizo, hitaji ambalo Jumatatu ya wiki iliyopita iliwasilisha ombi rasmi la kupewa takwimu hizo, lakini hadi jana taarifa hizo hazijajibiwa.Tangu kuingia madarakani, Rais John Magufuli amekuwa mstari wa mbele katika kufuatilia ukusanyaji wa fedha za serikali kutokea kwenye miradi yake mbalimbali. Hakusita kutoa neno kuhusu uuzwaji wa nyumba hizo za serikali na kutaka ufuatiliwe, ili wababaishaji wa aina hiyo ambao hawajalipa, wachukuliwe hatua.Waliouziwa nyumba hizo, waliuziwa bila ya kuwapo kwa nyongeza ya asilimia yoyote kwa maana ya fedha ya faida, ila licha ya kuwa nyingi zilikuwa kwenye maeneo muhimu ya kibiashara.Hata hivyo, wapo hao ambao hawajamalizia kuzilipa. Mkataba kwa waliouziwa nyumba hizo, hawakutakiwa pia hata kufanya matengenezo makubwa; na kama kulikuwa na haja ya kufanya matengenezo makubwa ya nyumba hizo, walikuwa wakitakiwa kupewa kibali kutokea TBA.Kwa mujibu wa Tarimo, TBA inao uwezo wa kumnyang’anya nyumba mtu aliyekiuka mkataba huo. Gazeti hili litaendelea kufuatilia kwa kina takwimu hizo kutokea TBA ili kuwabainisha ambao hawajalipa fedha hizo na kukiuka masharti ya kubadilisha matumizi. Katika mitaa mbalimbali hasa jijini Dar es Salaam kama vile Oysterbay, Masaki na Upanga, kuna maghorofa mengi ya kisasa ambayo yamepangishwa kwa shughuli za kiofisi, huku mengine yakitumiwa kama makazi ya kuishi kwa wageni na hata Watanzania, pia huku kwa asilimia kubwa kodi yake inatozwa kwa Dola ya Marekani.
3
Azam iliyokuwa ikishiriki michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF CC), juzi ilitupwa nje ya michuano hiyo baada ya kufungwa mabao 3-0 na Esperance ya Tunisia katika mechi ya marudiano ya raundi ya pili iliyochezwa mjini Tunis.Matokeo hayo yanaifanya Azam itolewe kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya kushinda mabao 2-1 katika mechi ya kwanza iliyofanyika Dar es Salaam Aprili 10, mwaka huu. Akizungumza jana, Dk Msolla alisema Azam haikuwa na maandalizi ya kutosha, ilicheza mechi chache za ligi ndipo ikaenda kucheza na Esperance wakati wapinzani wao walijiandaa muda mrefu.“Maandalizi ya zimamoto yaliiponza Azam, wenzetu walijiandaa muda mrefu na walijua kwamba wanacheza na walijua kwamba wanacheza na timu iliyowafunga mechi ya kwanza,” alisema. Dk Msolla alisema kingine kilichoiponza Azam ni kukosekana umakini kwa wachezaji wa timu hiyo, jambo ambalo lilifanya kufungwa mabao mepesi. “Timu haikuwa na mawasiliano, ikafungwa mabao mepesi, wachezaji walimuacha Bocco (John) peke yake muda mrefu, hivyo mabeki wa Esperance walipenya wanavyotaka,” alisema.Naye Grace Mkojera anaripoti kuwa nahodha msaidizi wa Azam FC, Himid Mao, amewataka mashabiki wao kutokata tamaa baada ya kutolewa na Esperance ya Tunisia.Kwa mujibu wa tovuti ya Azam FC, Mao aliyeingia dakika ya 79 katika mchezo huo kuchukua nafasi ya Salum Abubakar ‘Sure Boy’, alisema kwa sasa nguvu zao zote wanahamishia katika Ligi Kuu soka Tanzania Bara na Kombe la FA, akiwaahidi kuwa watapambana kuchukua makombe yote hayo.“Matokeo yamewasikitisha watu wengi hasa sisi wachezaji, lakini wanatakiwa wajue Azam FC ni timu changa sana na kwa sasa tunapiga hatua kubwa, lakini hii haitufanyi tuvimbe vichwa kwani bado tuna deni. “Hivyo nafikiri inabidi tufanye kitu kikubwa zaidi kuweza kusogea na wao mashabiki waendelee kutupa sapoti, bado ligi ipo, FA ipo tutajitahidi kuweza kuchukua makombe yote hayo. “Mchezo ulikuwa mgumu, ulikuwa mzuri dakika 45 za kipindi cha kwanza, tuliweza kuikabili presha ya ugenini na hatukuweza kuruhusu bao, kipindi cha pili naona wenzetu walirudi na nguvu zaidi, tulizuia wakapata mabao kutokana na labda makosa yetu ya kiuchezaji wakaweza kushinda,” alisema.Mao alisema ni hatua kubwa wamefikia mpaka sasa hadi kutolewa hasa kutokana na ukubwa wa wapinzani wao waliokuwa wakipambana nao.“Unajua mpira ni mchezo wa makosa na katika mpira unajifunza kila siku iwe unacheza mechi au unafanya mazoezi, ukiiangalia Esperance ipo kwenye nafasi za juu Afrika (nafasi ya tatu), ni timu nzuri ni timu bora, sisi kufika hapa na namna tulivyocheza na hatua kubwa sana tumefika, lakini ni changamoto kwetu inabidi tuchukue kitu ambacho kitatusaidia kufanikiwa katika mashindano yanayokuja mbele,” alisema.Azam FC iliyopanda Ligi Kuu miaka minane iliyopita, msimu huu ilikuwa ikishiriki kwa mara ya nne michuano ya Afrika hadi inafika raundi hiyo ilifanikiwa kuwatoa Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 7-3.
4
VINARA wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Yanga leo wanashuka dimbani kwenye Uwanja wa CCM, Kambarage Shinyanga kusaka pointi tatu katika mchezo dhidi ya Stand United. Yanga na Stand United mara ya mwisho kukutana ilikuwa raundi ya kwanza zilipofungana mabao 4-3 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa.Kipa Klaus Kindoki hatosahau mchezo huo uliompa presha kubwa akionekana kushindwa kumudu hali iliyosababisha baadhi ya mashabiki kumponda kwa kufungwa mabao kizembe. Kwa mara nyingine anakutana nao huenda akawa makini zaidi awamu hii kwani tayari amepata uzoefu baada ya kufanya vizuri katika mechi zilizopita. Yanga pia, haitamsahau mshambuliaji wa Stand Alex Kitenge aliyewafunga ‘Hat trick’ katika mchezo wa raundi ya kwanza.Bila shaka mchezaji huyo anahitaji kuchungwa. Stand United licha ya kuwa ina wachezaji wengi wazuri wa ndani na nje ya nchi, haiko katika mwenendo mzuri. Katika michezo 21, imeshinda sita, sare tatu na kupoteza 12 ikishika nafasi ya 17 kwa pointi 21.Ikipoteza mchezo wa leo basi itazidi kujiweka kwenye hatari ya kushuka daraja hivyo, inahitaji kupambana kujiondoa ilipo. Inakutana na Yanga iliyoko vizuri kileleni kwa pointi 53 ikiwa na rekodi ya kutopoteza mchezo wowote katika michezo 19, ikishinda 17 na kupata sare mbili. Timu hiyo ya Jangwani imekuwa ikifanya vizuri kwenye uwanja wa nyumbani na hata ugenini.Je, itaendeleza rekodi hiyo au itavunjwa? Mechi nyingine itakayochezwa leo ni Azam FC dhidi ya Mwadui, ikitarajiwa kuwa na kisasi baada ya ule uliopita wa raundi ya kwanza kutoka sare ya bao 1-1 ugenini mkoani Shinyanga.Azam FC imeshindwa kufanya vizuri katika mchezo uliopita wa ligi dhidi ya Ruvu Shooting ikitoka kupata sare ya bila kufungana 0-0 na kuzidi kuipa Yanga nafasi ya kubaki kileleni kwa pointi nyingi.Timu hiyo inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi 41, tofauti ya pointi 12 dhidi ya Yanga inayoongoza. Imeshacheza michezo 18, imeshinda 12, sare tano na kupoteza mmoja.Mchezo wa leo ni muhimu kwao kushinda kuendelea kuwa katika mbio za ubingwa wa ligi. Mwadui inashika nafasi ya 11 ikiwa na pointi 24, imecheza michezo 22, imeshinda sita, sare sita na kupoteza 10. Ikipoteza itakuwa kwenye nafasi ya kushuka zaidi chini hivyo, inahitaji ushindi ili kupanda katika nafasi za juu
4
NA KULWA MZEE DAR ES SALAAM MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeombwa kuamuru Mchungaji Joseph Mwingira wa Kanisa la Efatha, mke wa mtu anayedaiwa kuzaa naye, mtoto na mume halali wakapime DNA ili kujua mtoto ni wa nani. Maombi hayo yametokana na kesi dhidi ya Mwingira, anadaiwa kuzini na kuzaa na  Dk. Phillis Nyimbi ambaye ni mke wa Dk. William Morris ambaye ni raia wa Marekani amewasilisha maombi mahakamani kwa sababu anadai wawili hao walizini wakazaa mtoto huyo mwenye umri wa miaka tisa sasa. Morris kupitia wakili wake Respicius Ishengoma aliwasilisha maombi hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, katika maombi hayo namba 113/2017, ambapo baada ya kuwasilisha maombi hayo mahakama imeyapokea na kutoa siku 14 kwa Mwingira kuyajibu kisha usikilizwaji wa maombi uanze na kutolewa uamuzi Agosti 2, mwaka huu. Katika kesi ya msingi namba 306/2013 Morris amewashtaki Mwingira na mkewe Dk. Phillis, anadai alipwe fidia ya Sh bilioni 7.5 kwa Mwingira kuzini na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mkewe. Mdai anadai Dk. Nyimbi na Mwingira waliingia katika mahusiano katika muda usiojulikana bila kujali kwamba Nyimbi alikuwa mke wa mdai katika kesi hiyo. Inadaiwa katika uchunguzi Dk. Nyimbi alidai alibakwa na Mwingira ambapo kubakwa kulisababisha kupata ujauzito na matatizo mbalimbali ya kiafya. Mdai alifunga ndoa ya kanisani na mkewe Nyimbi Desemba 28 mwaka 2011. Mchungaji Mwingira na Nyimbi waliingia katika mahusiano ya mapenzi na kubahatika kuzaa mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 9 sasa.
3
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema hatua ya kudhibiti upotevu wa mapato na matumizi ya fedha za serikali, uboreshwaji wa mazingira ya biashara na uwekezaji na kusimamia uwajibikaji kwa watumishi wa umma, vimewezesha kukua uchumi.Amesema Tanzania ni nchi yenye amani na utulivu na serikali imeendelea kuongeza nguvu katika kudumisha amani na utulivu kwenye maeneo yote nchini, hali inayotoa fursa kwa wananchi wake kuendeleza shughuli zao za maendeleo.Waziri Mkuu alisema hayo jana alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Misri, Dk Mostafa Madbouly katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi nchini Misri.Hivyo, alimhakikishia Waziri Mkuu wa Misri kwamba serikali ya Tanzania na wananchi wake, wapo tayari kuendelea kushirikiana na serikali ya nchi hiyo na wananchi wake katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi hizo mbili.Alisema nchi za Tanzania na Misri, zinahitaji kutumia nafasi ya ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji katika ukuzaji wa uchumi, hivyo aliwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Misri waje kuwekeza nchini.Alisema serikali ya Tanzania imefanikiwa kiuchumi na kwa sasa ni nchi ya pili ambayo uchumi wake unakua kwa kasi barani Afrika, ikitanguliwa na Ivory Coast.Uchumi wa Tanzania ulitarajiwa kukua kwa asilimia 7.2 mwaka jana kutoka asilimia saba.“Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea vizuri, tumeendelea kushuhudia kushuka kwa mfumko wa bei ambapo kwa sasa tumefikia asilimia 3.2, kiwango hiki ni matokeo ya kukuza sekta za madini, ujenzi, mawasiliano, utalii pamoja na kushuka kwa bidhaa za chakula na mafuta. Tunatarajia kiwango hiki kitashuka zaidi kwa sababu ya uwekezaji,” alieleza.Waziri Mkuu alisema Serikali ya Awamu ya Tano tangu ilipoingia madarakani mwaka 2015, kipaumbele chake kilikuwa ni kukuza kiwango cha uchumi kutoka cha chini kwenda cha kati ifikapo mwaka 2025 kupitia sekta ya viwanda.
5
BAADA ya kutokea tafsiri na uelewa tofauti kuhusu wagombea wanaopaswa kushiriki uchaguzi mkuu wa Novemba 24, mwaka huu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo amesema watakaowania nafasi za uongozi ni wale walioteuliwa na pingamizi na rufaa zao zimekubaliwa.Wakati hayo yakijiri, baadhi ya vyama vya siasa, vimetoa masharti ya kufuatwa ili vishiriki uchaguzi huo. Vimetoa kauli hiyo baada ya Waziri Jafo, kutoa kauli ya kuwarejesha wagombea wote kwenye kinyang’angiro cha uchaguzi huo unaofanyika Novemba 24, mwaka huu.Hata hivyo, baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs), yamewataka viongozi wa vyama vya upinzani nchini, kutafakari upya kuhusu kitendo walichokifanya cha kususia uchaguzi wa serikali za mitaa, kwamba uamuzi huo unavunja demokrasia.Kuhusu tatizo la tafsiri juu ya tamko lake, Jafo alieleza kuwa “ Ili kuondoa tofauti ya uelewa ambao mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa za mwaka 2019, ufafanuzi watakaowania uongozi huo ni wale wenye sifa.”Jafo alibainisha kuwa watakaoshiriki uchaguzi ni waombaji wote ambao walichukua na kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa, kugombea nafasi za uongozi na kisha wakateuliwa na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi.Alisema pia ni waombaji wote waliowasilisha pingamizi kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi, kuomba kuteuliwa na pingamizi zao zilikakubaliwa.Jafo alisema pia ni wale waombaji wote, waliokata rufaa kwenye Kamati za Rufaa za Wilaya na rufaa zao kukubaliwa.Kutokana ufafanuzi huo, ina maana wataopata fursa ya kuwania nafasi za uongozi ni walioteuliwa, pingamizi zao kukubaliwa na wale 4,921 ambao rufaa zao zilikubaliwa, ambazo ni asilimia 32 ya rufaa 15,380 zilizokuwa zimepelekwa kwenye kamati.Awali, bungeni wakati akijibu mwongozo kuhusu masuala ya uchaguzi wa serikali za mitaa, waziri huyo alizima hoja mpya ya wapinzani, waliotaka Kauli ya Serikali kwa wagombea ambao wameshindwa kurudisha fomu.Alisisitiza kuwa anaona sasa, wamehamisha goli.Jafo alitoa kauli hiyo baada ya Spika Job Ndugai, kumpa fursa kutoa ufafanuzi, baada ya Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma (CUF) kuhoji kauli ya serikali kwa wagombea walioshindwa kurejesha fomu.Mwongozo Awali, Mbunge Nachuma alisimama kwa kufuata Kanuni za Bunge na kutoa hoja ya kutaka mjadala wa Bunge, unaoendelea uahirishwe ili kujadili suala la uchaguzi wa serikali za mitaa. “Bado kuna mambo hajayataja waziri hajayafafanua vizuri juzi, mfano wa mambo hayo ni baadhi ya maeneo kama Liwale, asilimia 99 ya wagombea wa upinzani hawakupewa fomu na maeneo mengine.“ Kuna baadhi ya maeneo Kamati za Siasa za CCM, zilikuwa zinawajazia watu fomu usiku ili waonekane wamejaza mara mbili ikiwemo Mtwara Mjini, Mheshimiwa Spika naomba busara yako iweze kutumika ili tutumie dakika 30 kujadili, kwa sababu huko kuna mambo ya hatari”alitoa hoja Nachuma.Kutokana na hoja yake kutoeleweka, Spika Job Ndugai alimtaka kueleza anataka serikali ifafanue nini hasa.Nachuma alisema pamoja na kuwa Jafo alitoa maelekezo ya wale walioondolewa, kurejeshwa kushiriki uchaguzi, lakini suala la wale walioshindwa kurejesha fomu, linatatuliwaje.“Nilichokuwa nikihitaji haya manyanga ambayo yamefanyika, kwa makusudi ya kuwanyima wapinzani fomu, kuna wagombea wetu fomu zimekataliwa, naomba Jafo azungumze na serikali inatoa kauli gani” alisema. Kutokana na mwongozo huo, Spika Ndugai alitoa fursa kwa Jafo kutolea ufafanuzi suala hilo.Akifafanua, Jafo alisema: “Sisi wote ni Watanzania, inawezekana tunatofautiana nia, kwa ufafanuzi nilioutoa jana (juzi) kwa watu wote waliochukua na kurudisha fomu, sasa watu wote wakacheze demokrasia uwanjani...”“Lakini tunahamisha goli tena, sina comment zaidi ya hiyo. Kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu ipo siku wataenda kujibu haki mbele ya Mwenyezi Mungu. Nadhani kwa hekima iliyofanyika, ni binadamu wachache watatafsiri nini nia ya watanzania hao.Jafo aliongeza: “Mheshimiwa Spika jambo langu ni hilo tu, kama kweli watu wana hofu ya Mungu walikuwa wanasema kwamba watu wamekatwa bado watu wanahamisha goli, Mheshimiwa Spika ‘I have no more comment.”Aidha, taasisi isiyo ya kiserikali ya Aliance for Development Organization (ADO) , iliwataka viongozi wa vyama vya upinzani nchini, kujitafakari upya kuhusu kitendo walichokifanya cha kususia uchaguzi wa serikali za mitaa kwamba uamuzi huo unavunja demokrasia.Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwakilishi wa ADO, Ally Mwinyi alisema kitendo cha kujitoa kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa, kinadhoofisha demokrasia na kuwanyima haki wananchi ya kuchagua viongozi wanaowataka.Pia alisema kitendo cha baadhi ya vyama vya siasa kutoa tamko kabla ya majibu ya rufaa zao kutolewa, si picha nzuri kwa maendeleo ya demokrasia, kwa sababu walitakiwa wawe wavumilivu hadi hapo rufaa zao zitakaposikilizwa na kutolewa majibu.Aliongeza kuwa vyama vya siasa vinatakiwa kuheshimu demokrasia na kuwa mstari wa mbele, kuonesha katika kupigania ukuaji wa demokrasia nchini.Mwanaharakati wa mambo ya kijamii, Mackdeo Shilinde, amesema kuwa uchaguzi huo utakaofanyika Novemba 24, mwaka huu, unatakiwa ufanyike kwa amani na haki ambayo inapaswa kuanzia kwenye vyama, wagombea na wananchi ili waweze kuchagua kiongozi wanayemtaka.Kwa upande wa vyama vya upinzani, Mwenyekiti wa Kampeni na Uchaguzi Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo, Joran Bashange alisema ili warejee kwenye uchaguzi ni lazima masharti yao matano yafuatwe.Masharti hayo ni moja mchakato wote wa uchaguzi, uanze upya hasa kwa yale maeneo yaliyofanywa chini ya utaratibu wa sasa yafutwe kwanza. Aliongeza kuwa pia itabidi kwanza zitungwe kanuni mpya za uchaguzi kwa maridhiano na makubaliano na vyama vya siasa.Pia kuundwe kamati huru ya kusimamia uchaguzi, itakayoridhi kwa pamoja makubaliano ya chama na sio Tamisemi, kwa kuwa sio huru.Bashange alilitaja agizo jingine kuwa ni kufanyika kwa kikao cha pamoja cha vyama vyote vya siasa, kwa lengo la kukubaliana juu ya namna ya kusonga mbele kwa utekelezaji wa mapendekezo kwa vyama vya siasa.Suala la tano ni kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi, itakayosimamia chaguzi zote kuanzia huu na ule wa mwakani.Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Vicent Mashinji alisema Kamati Kuu ya chama hicho, imeshaamua kuwa haiwezi kushiriki uchaguzi huo, kwa kuwa umejaa dhuluma na kuwa hata mgombea atakayeshiriki, hatatambuliwa na chama.Imeandikwa na Anastazia Anyimike, Dodoma na Evance Ng’ingo na Francisca Emmanuel, Dar
3
Anna Potinus – Dar es Saalam Rais Dk John Magufuli amekemea vikali vitendo vya ubakaji vinavyoendelea Mkoani Mbeya, amewataka viongozi na wananchi kushirikiana kwa pamoja kutokomeza tatizo hilo kwa kuwachukulia hatua wanaohusika na vitendo hivyo. Ametoa kauli hiyo Jumamosi Aprili 27, wakati akizungumza na Wananchi wa wilaya ya Chunya mkoani humo katika ziara yake ya kikazi ya siku nane ambapo ameshazindua barabara ya Mbeya – Chunya yenye urefu wa kilomita 72 na kuweka Jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Chunya – Makongorosi. Dk Magufuli amewataka viongozi hao kuiga mfano wa marehemu Abbas Kandoro kwa namna alivyosaidia kwenye hukumu ya mwanaume aliyehukumiwa kifungo cha maisha kutokana na kupatika ana hatia ya kulawiti mtoto ambaye hadi sasa yupo katika hali mbaya. “Tatizo la ubakaji linaonekana linataka kuwa ugonjwa katika maeneo haya, jana kuna mama alijitokeza katika mkutano wetu akaeleza shida yake kwamba ana mtoto wake ambaye alilawitiwa akiwa na miaka sita kukawa na ujanja ujanja na baadaye alienda kumuona aliyekuwa Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro akaishughulikia kesi hiyo vizuri na hakimu akatumia sheria zote na mtuhumiwa akahukumiwa kifungo cha maisha,” amesema. “Nitoe wito kwa viongozi kuiga mfano wa Mzee kandoro maana alisimamia haki popote palipokuwa hakuna haki, hivyo yeyote atakayefanya vitendo vya ajabu apelekwe kwenye vyombo vya dola na nina imani tukilisimamia hili kwa pamoja tutazaa matunda mazuri,” amesema. Aidha ametoa agizo kwa viongozi mkoani huo kuhakikisha wanafungua soko la madini katika Wilaya ya Chunya ndani ya siku saba na kwamba hilo ndilo litakuwa jaribio lao kubwa licha ya kuwa na utendaji mzuri mkoani humo. “Kama Mkuu wa Mkoa wa Geita ameweza kufungua soko la madini wakuu wa mikoa mingine mnashindwa nini? Tunatoa mateso kwa wananchi hawa mkuu wa mkoa na viongozi wengine hili ndilo jaribio lenu na mnalipwa kwa wakati, magari mnayo sasa ndani ya siku saba mjipange wenyewe ili wananchi hawa wachimba dhahabu wapate maeneo ya kuuzia dhahabu zao,” amesema. “Nilichaguliwa kusema ukweli na hili agizo sio la mkuu wa mkoa wa Mbeya peke yake siwezi kuwa na wakuu wa Mikoa ambao ninatoa agizo halafu hawatekelezi hawa wananchi ndio walionichagua mvua zikiwa zinanyesha, jua linawaka wakaniambia nikafunge makufuli yote hivyo achana na hizo dhambi za kutamani, kamilisha kwanza hili la kuanzisha soko hapa ndio ukatamani halafu ukimaliza ukatubu dhambi zako,” amesema Dk Magufuli huku wengi wakiangua kicheko.
3
BAADA ya Simba kuvurunda katika michezo miwili mfululizo ya Ligi ya Mabingwa Afrika, mchezaji nguli wa zamani wa timu hiyo, Abdallah Kibadeni amejitokeza na kuitaka timu yake hiyo ijitafakari huku akieleza wazi inachokifanya kwa sasa hakipendezi na kinahuzunisha.Kibadeni aliyewahi pia kuwa kocha wa timu hiyo, amezungumza hayo baada ya mwishoni mwa wiki iliyopita, Wekundu hao wa Msimbazi kufungwa mabao 5-0 dhidi ya Al Ahly ya Misri, ikiwa ni mchezo wa pili wanapoteza kwa idadi hiyo ya mabao baada ya ule wa Kinshasa Congo DR dhidi ya AS Vita.“Kinachotokea kwa sasa pale Simba hakipendezi hata kidogo, wala hakileti faraja yoyote. Ijitafakari kwa kweli na iangalie kiufundi hasa pamoja na benchi lake la ufundi, shida ni nini na kwa nini inakuwa hivi.“Maana hatuwezi jua kitu gani kule ndani ya timu kinaendelea lakini kwa nje ukiiangalia Simba ni kama timu ambayo imeridhika na mpaka leo imelewa ushindi wa 3-0 walioupata katika mechi ya kwanza dhidi ya JS Saoura (Algeria) nyumbani.“Nafikiri kocha na wachezaji wake waangalie mapema cha kufanya, maana wale Al Ahly walicheza mechi yote peke yao, waliamua kutufunga kipindi cha kwanza na cha pili wakatulia tu na si kwamba walishindwa kufunga mengine isipokuwa waliamua kupumzika tu, sasa hiyo siyo nzuri,” amesema Kibadeni.Zamoyoni Mogella aliyewahi kuwika na timu za Simba na Yanga miaka ya nyuma naye aliamua kueleza anachokiona juu ya mwenendo huo wa Simba, timu pekee inayoiwakilisha Afrika Mashariki katika michuano hiyo mikubwa zaidi Afrika kwa ngazi ya klabu.“Sijui nini kinatokea lakini katika hii mechi wachezaji hawakuwa mchezoni. Matokeo haya yanasikitisha maana timu inafungwa mabao 10 katika mechi mbili, sasa sijui nini kipo pale Simba kama tatizo ni kocha au wachezaji, haieleweki.“Sijui itakuwaje marudiano maana tunacheza nao tena baada ya wiki moja, sasa sijui hii morali ya ushindi wa hapa nyumbani unaitengenezaje. Nafikiri kuna muda hata wachezaji nao wanapaswa kujiongeza maana ukiacha mbinu za kocha hata wao watumie maarifa yao kupata ushindi maana wao ndiyo wanaaibika zaidi,” alisema.
4
WAJUMBE wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar imekiri kujifunza mambo makubwa katika ujenzi wa jengo la Tatu la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3).Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mohammed Said amesema ujenzi wa jengo hilo ni fundisho tosha kutokana na kwenda kwa kasi tangu ujenzi wake uanze Juni,  2013, tofauti na ujenzi wa jengo la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Amani Abeid Karume umechukua takribani miaka 10, tangu mwaka 2009 lakini hadi sasa lina asilimia 39 pekee.Mhe. Said amesema TB3 ni jengo la kisasa kutokana na miundombinu yake ambayo mingi inaendeshwa kwa mifumo maalum, ikiwemo sehemu ya mizigo, ambayo inaendeshwa kupitia hatua tano.“Katika ziara hii tumefarijika sana kwani tumejifunza mengi wenzetu walivyoweza kuufikisha mradi huu, kwa kweli tumechukua yote na tutakwenda kuishauri serikali namna bora ya kuendeleza ujenzi wa majengo na viwanja vya ndege kwa ujumla,” amesemaSaid ambaye ni Mwakilishi wa Mpendae.Hali kadhalika, Mwenyekiti Said amesema mbali na kutembelea jengo hilo, pia wamepata maelezo mazuri ya kiutendaji katika uendeshaji, ukusanyaji na mgawanyo wa mapato kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), na wataishauri serikali namna bora ya kudhibiti mapato.Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Lawrence Thobias, ameishukuru kamati hiyo kwa kuichagua TAA kuwa sehemu yake ya mafunzo, kwa kuwa imezoeleka wengi wanaotaka kujifunza lazima waende nje ya nchi. Thobias amesema TAA ikiwa ni moja ya taasisi za serikali chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, imekuwa ikijiendesha kwa kufuata sheria na taratibu za ukusanyaji wa mapato za serikali.Akiwasilisha maendeleo ya mradi wa jengo la tatu la abiria, mmoja wa wasimamizi kutoka Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Burton Komba amesema hadi kufikia Oktoba 31, 2018 umefikia asilimia 85.53 na unatarajiwa kukamilika Mei 2019.Mhandisi Komba amesema ujenzi wa jengo hilo ambalo litahudumia abiria milioni sita kwa mwaka, umehusisha eneo la maegesho ya ndege lenye mita za  mraba 227,000 lenye uwezo wa kuegesha ndege 19 za Daraja C kwa wakati mmoja zikiwa kwenye madaraja na eneo lisilokuwa na madaraja.“Pia eneo hili linaweza kuegesha ndege za daraja E 11 mfano wa hii Dreamliner ya ATCL Boeing 787 na Boeing 777, ni eneo kubwa,” amesema.Pia amesema kumejengwa maegesho ya magari mchanganyiko yasiyopungua 2075 kwa wakati mmoja; barabara za kuingia na kutoka eneo la jengo; uzio wa usalama, mifumo ya maji taka nay a mvua; ujenzi wa matanki ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita milioni 2.26; kituo kikubwa cha umeme (33Kv); usimikaji wa jenereta saba zenye uwezo wa KvA 2000 kila moja; ujenzi wa mifumo ya kujaza mafuta kwenye ndege na kusimika mifumo ya mawasiliano na usalama.
3
Pia Lwandamina alisema jana Dar es Salaam wiki moja inamtosha kuandaa kikosi chake kwa msimu mpya wa ligi na Ligi Kuu ya Tanzania Bara ambayo imepangwa kuanza Agosti 26 mwaka huu.Programu ya Lwandamina ilianza kwa mazoezi ya wachezaji kutanua misuli ya miili kwa wiki moja katika Gym City Mall. Juzi wachezaji waliingia hatua ya pili ya mazoezi ya uwanjani kufundishwa vitu mbalimbali ikiwemo mbinu na mifumo.Alisema kitu alichopanga kuanza nacho ni kutengeneza mfumo wa uchezaji ambao ni muhimu kuipa timu matokeo mazuri. Alisema ataiunganisha timu kiuchezaji kwani baadhi ya wachezaji ni wageni hivyo wanatakiwa kuelewana na msimu uliopita.Yanga leo wanaenda Morogoro kupiga kambi ya wiki moja kujiandaa dhidi ya Simba mechi ya Ngao ya Jamii Agosti 23. Katika kujiimarisha zaidi jana wamemsajili kipa wa Serengeti boys, Ramadhan Kabwili ambaye ataungana na makipa wengine wawili.Watacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida United Agosti 6 Uwanja wa Taifa. Msemaji wa Yanga, Dismas Ten alisema Lwandamina amepania kuweka rekodi hivyo anahitaji mazingira yaliyotulia. Simba wako Afrika Kusini kujiandaa na msimu tangu wiki iliyopita.
4
KOCHA wa timu ya Azam FC, Mholanzi Hans van Pluijm (pichani), amesema kuwa wachezaji wake walitengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini walishindwa kuzitumia.Pluijm aliyasema hayo baada ya kumalizika kwa mchezo wa Kombe la Mapinduzi kati yake na timu ya Jamhuri, ambapo walilazimishwa sare ya kufungana bao 1-1. Alisema kuwa katika mchezo huo vijana wake, ambao ndio mabingwa wa Kombe la Mapinduzi, walijitahidi kucheza vizuri, licha ya kuuanza mchezo taratibu.Alifahamisha kwamba huu ni mchezo wao wa kwanza ambao walipaswa washinde ili kujiweka katika mazingira mazuri, lakini wamejikuta wakipangwa na kulazimishwa sare, na sasa wanajipanga kwa ajili ya mchezo ujao. “Hii ni mechi yetu ya kwanza pamoja na kwamba tulipaswa kushinda, lakini tumetoka na pointi moja tunajipanga kwa michezo iliyo mbele yetu”, alisema kocha huyo. Hata hivyo, alisema kuwa pamoja na yote hayo lakini wachezaji wake walicheza kwa kupooza na kushindwa kuzitumia nafasi walizozipata.Azam ambao ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo kwa mara mbili mfululizo wanatarajiwa kushuka dimbani kesho kucheza na Yanga, mchezo ambao utapigwa kuanzia majira ya saa 2:15 usiku.Azam FC ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika mchezo huo uliokuwa na msisimko wa hali ya juu kwa kupata bao katika dakika ya 28, lililopachikwa na Tafadzwa Kutinyu, kwa mkwaju wa penalti baada ya Emmanuel Balele, kuunawa mpira wakati akiokoa shuti la mfungaji wa bao hilo. Jamhuri iliyocheza kwa nidhamu kubwa kwenye eneo la ulinzi hadi kufanikiwa kuwabana washambuliaji wa Azam FC, ilipata bao la kusawazisha katika dakika ya 66 lililofungwa na Abdul Ramadhan, na kutoka na pointi moja.
3
ALIYEKUWA Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Makerere, Dk Dan Okello aliyeishtaki serikali kwa madai ya kushindwa kuongeza ufadhili katika sekta ya kilimo, ametangaza nia ya kugombea urais katika uchaguzi ujao.Okello aliliambia gazeti la Daily Monitor kuwa anajiandaa kushindana na Rais Yoweri Museveni katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021. “Tunataka fedha zaidi katika kilimo ili kununua trekta na ng’ombe wa kulimia, tutajenga mabwawa katika kila kijiji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji, ndiyo maana nataka kugombea urais,” alisema.Dk Okello, aliyekuwa Mwenyekiti wa Wlaya ya Lira katika Chama cha upinzani cha Uganda People’s Congress (UPC) kwa miaka 20, kwanza anatakiwa kuchaguliwa na chama chake kama mgombea wake kabla ya kushindana na Museveni.“Natarajia kuwa mgombea kwa chama cha UPC kwa sababu Uganda yote watu wananisubiri kuwa rais anayefuata wa UPC, hivyo moja kwa moja nitakuwa mgombea wa chama hiki katika uchaguzi mkuu ujao,” alisema. Alisema tayari amehamasisha wakulima kuchagua UPC katika uchaguzi ujao kwa kuipeleka serikali ya NRM mahakamani. Mwaka jana, Dk Okello alifungua kesi dhidi ya Mwanasheria Mkuu katika Mahakama Kuu ya Lira kwa serikali kushindwa kuelekeza asilimia 10 ya bajeti ya serikali katika sekta ya kilimo.
3
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mhandisi Mshamu Munde anajivunia namna alivyojenga umoja wa watumishi unaowezesha kuongezeka kwa kasi ya kuvuta wawekezaji.Amesema ofisini kwake mjini Mkuranga kuwa, ameratibu watumishi, wanafanya kazi kama timu na hawategemei ujuzi au umahiri wa mtu mmoja kufanikisha malengo yao.“Hata mimi mwenyewe sio kitu ambacho ninaweza nikasema najivunia umahiri wangu binafsi. Nimejenga timu, tunaaminiana lakini pia tumeongeza ili kasi ya kuvuta wawekezaji baada ya kuunda hii timu ya uwekezaji ambao baada ya kupeana hadidu za rejea nini kifanyike ili mwekezaji akija hapa asitoke kwenda kwingine”amesema Munde.Ameyasema hayo wakati akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) waliopo Pwani kuzitangaza fursa za biashara na uwekezaji mkoani humo.Munde amesema, ameunda Kamati ya Uwekezaji inayojumuisha Ofisa Mipango, Ofisa Biashara, Ofisa Ardhi, Mwanasheria, na Ofisa Maendeleo ya Jamii.“Ofisa Maendeleo ya Jamii ana uwezo wa kuongea na jamii kwa sababu kwenye uwekezaji kuna mambo mawili. Ukishamuita mwekezaji ukampa profile ya halmashauri lakini ukamuelezea miundombinu wezeshi iliyopo kwenye halmashauri na kama uwekezaji huo umelenga kwenye kata fulani au tarafa fulani tunatarajia ile Kamati ya Uwekezaji iende ikatoe hamasa kwa wananchi kwa sababu sio kila mwananchi anaelewa hii dhana ya uwekezaji”amesema.Munde amesema hadi sasa hawana miradi ya kimkakati lakini wapo kwenye mchakato wa kujenga miradi kadhaa ukiwemo wa kujenga kituo cha mabasi yaendayo mikoa ya kusini katika eneo la Mwandege, na kujenga soko la samaki Kisiju.
3
JUMLA ya wanawake 50,000 hapa nchini kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), hupata maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi na hivyo kusababisha asilimia 37 ya wanawake wanaogundulika na ugonjwa huo kufariki dunia kila mwaka.Hayo yalisemwa juzi jijini hapa na Ofisa Mpango wa Chanjo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Pricella Kinyunyi alipokuwa akieleza lengo mahususi la serikali kuanzisha chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi. Ofisa huyo alikuwa akizungumza na wasichana wenye umri kuanzia miaka 9 hadi 14 kwenye mkutano wa wadau wa sekta ya afya kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza.Alisema wagonjwa wengi wa saratani ya mlango wa kizazi hawapati mapema huduma za ugunduzi na matibabu sahihi kwa wakati hali inayosababisha vifo. “Takwimu kutoka Hospitali ya Ocean Road inaonesha kwamba saratani ya mlango wa kizazi inachangia kwa asimilia 36 ya saratani zote na asilimia 70 ya wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi wanajitokeza katika hatua ambayo tayari saratani imeshasambaa maeneo mengine mwilini,”alisema.Alisema chanjo hiyo ya saratani ya mlango wa kizazi ni salama na imethibitishwa na WHO na kwamba majaribio ya matumizi ya chanzo kwa mara ya kwanza yalianzia mkoani Kilimanjaro mwaka 2014 na haikuwa na madhara ya kiafya. “Matokeo ya chanjo hiyo yalikuwa ni mazuri, mkoa ulifikia asilimia 90 ya uchanjaji, lengo hasa lilikuwa ni kupata uzoefu wa kujifunza kwa vitendo kabla ya kwenda nchi nzima,”aliongeza.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela katika kuhakikisha ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi unatokomezwa, aliwataka wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji na wenyeviti wa halmashauri kuhakikisha wanahamasisha vijana wengi kwenye maeneo yao ili wapate chanjo hiyo.Kwa mujibu wa taarifa za serikali, mkoa wa Mwanza umetekeleza chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi iliyozinduliwa rasmi Aprili 23, mwaka jana na kuandikisha wasichana 31,291 wenye umri chini ya miaka 14, ambapo uliweza kuchanja wasichana 24,628 ikiwa ni sawa na asilimia 79 ya ufanisi.
3
PARIS, UFARANSA MATIBABU dhidi ya virusi vya Ukimwi (VVU) yanatarajiwa kutolewa kupitia sindano. Kwa mujibu wa wanasayansi, dawa hiyo itakuwa ikitolewa mara sita kwa mwaka. Wamesema kuwa kubuniwa kwa muundo huo mpya wa dawa ya VVU kutolewa kwa sindano, kunaweza kutoa tiba fanisi zaidi iwapo itapitishwa. Tiba hiyo ya sindano, ambayo huendelea kuingiza taratibu dawa ya VVU katika damu ya mgojwa, iko katika hatua ya pili ya majaribio. Dawa hiyo inatarajiwa kupunguza mzigo wa dozi za vidonge na kutoa ahueni kwa watu wanaoishi na VVU mara itakapopitishwa. Watu wengi huhangaika kumeza dawa kila siku na katika kesi nyingi husababisha VVU kurudi na kuwapo usugu dhidi ya dawa. Matokeo hayo yaliwasilishwa juzi Jumanne katika Mkutano wa Kimataifa wa Ukimwi kuhusu sayansi ya VVU mjini Paris, Ufaransa. “Kama utafiti wa dawa mpya ya kukabiliana na VVU, kufuata masharti ya tiba kunaendelea kuwa njia nzuri zaidi ya kukabili VVU na kupunguza usugu dhidi ya dawa,” alisema Dk. David Margolis, mtafiti kutoka taasisi ya ViiV Healthcare. Katika matokeo ya utafiti, kulikuwa na asilimia 94 ya kukabili virusi kwa wagonjwa waliowekewa mseto wa dawa mbili kila baada ya wiki nane. Wiki nne ziliripoti ufanisi wa asilimia 87 kulinganisha na asilimia 84 kwa wagonjwa waliotumia mseto wa dawa ya kumeza. “Hakukuwa na wagonjwa walioashiria kuwapo usugu wa VVU dhidi ya dawa, maumivu kutokana na sindano ndiyo yaliyoripotiwa zaidi. “Athari za dawa ikiwamo kuhara na maumivu ya kichwa, yalishuhudiwa katika makundi yote,” alisema. Utafiti mwingine ulihitimisha kwamba uanzishaji wa kinga za mwili kwa watu walioathirika kunaweza kuchelewesha kuzaliana kwa VVU mwilini, hasa baada ya kuvurugwa kwa tiba ya dawa za kumeza za kufubaza makali ya VVU (ARVs). Utafiti unaojulikana kama RV397 ulitaka kupata matibabu ambayo yanaweza kuzuia mizigo ya virusi bila ya haja ya kutumia ARVs kila siku. Wanasayansi walijaribu kuangalia athari za kinga za mwili za VRCO1  ili kutambua mabadilikio ya virusi kwa watu walioathirika na VVU na ambao wamekuwa katika tiba ya ARVs. VRCO1 ni kinga ya mwili, ambayo inazuia mashambulizi mengi yanayosababishwa na VVU. “Hiyo ni mara ya kwanza kwa kinga ya VRCO1 kutathminiwa kwa watu, ambao walianza dawa wakati wa maambukizo makali ya VVU,” alisema Dk. Trevor Crowell, aliyewasilisha utafiti huo.
2
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeagizwa kufanya ukaguzi wa kushitukiza kwenye mabasi ya abiria, kubaini yanayoendela kusafi risha barua, vifurushi na vipeto bila kuwa na leseni.Agizo limetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye. Alisema bado kuna baadhi ya mabasi yanayotoa huduma hiyo bila kuwa na leseni. Akifungua mkutano wa siku tatu wa Baraza la Wafanyakazi na Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Nditiye alisema pamoja na mwaka jana kupiga marufuku mabasi ya abiria ambayo hayana leseni kufanya biashara hiyo, bado yameendelea.“Mwaka jana nilipiga marufuku mabasi ya abiria, ambayo hayana leseni ya kufanya huduma ya kusafirisha barua, vifurushi na vipeto kuacha biashara hiyo, lakini nimebaini kuwa baadhi ya mabasi bado yanaendelea kufanya hiyo biashara. Ni marufuku kampuni ambayo inafanya huduma hiyo bila leseni na sheria inakataza,”alisema.Aliagiza TCRA kuhakikisha inafanya ukaguzi wa mara kwa mara na wa kushitukiza, endapo basi lolote litakamatwa likifanya shughuli hizo basi lichukuliwe hatua za kisheria.“Nawaagiza TCRA kufanya ukaguzi wa kushtukiza kwenye mabasi hayo, wanatakiwa kufanya mkama wenzao LATRA (Mamlaka ya Usafiri wa Ardhini) ambao wanaamka asubuhi na kwenda kufanya ukaguzi. Kampuni yoyote ikikutwa inafanya shughuli hizo kinyume na sheria, ichukuliwe hatua za kisheria haraka,”aliagiza.Aidha, Nditiye aliwataka wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania, kuongeza ufanisi na tija kwenye shirika lao ili kuongeza gawio serikalini na kuongezeka kipato cha wafanyakazi. Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Hassan Mwang’ombe alisema mwanzoni mwa mwezi ujao, shirika litaingia rasmi kutoa huduma kidijitali.Alisema tayari mifumo yote ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(Tehama), imefungwa na kuungaisha ofisi zote za shirika hilo la kuwa kwa sasa wapo katika majaribio.“Mwishoni mwa mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi ujao, Shirika la Posta Tanzania litaingia kiditijatili, tutakuwa tunatoa huduma zetu kwa mtandao, kwa sasa tuko katika majaribio , hivyo tutakuwa na App yetu,”alisema.Alisema pia shirika liko katika mkakati wa kufanya mabadiliko makubwa ya kimuundo na mfumo wa utendaji, ambao umelenga kuboresha shughuli kwa kufanya kazi kwa ujuzi na tija zaidi.
3
Aliongeza kuwa mbali ya kutekeleza dhamira hiyo Mfuko huo pia unakwenda sambamba na utekelezaji wa lengo la nne la Mpango wa Kukuza Uchumi Zanzibar (MKUZA II) la kuimarisha Sekta Binafsi lenye shabaha ya kuongeza upatikanaji wa mikopo kutoka asilimia 43.2 mwaka 2009 hadi kufikia asilimia 86.9 ifikapo mwaka 2015.Mfuko huo wenye thamani ya Sh bilioni 1.1 unatarajiwa kutoa mikopo kwa wananchi yakiwemo makundi mbalimbali kama vijana ambao ni pamoja na waliomaliza masomo katika vyuo na skuli za sekondari, wanawake, vijana waliotoka katika vituo vya kutolea wajasiriamali na makundi ya walemavu.Dk Shein aliwaeleza wananchi na wageni waalikwa katika hafla hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort iliyopo nje kidogo ya Mji wa Zanzibar kuwa kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka 2009/2010 asilimia 17.1 ya vijana Zanzibar hawana ajira.“Hatuwezi kupata maendeleo ya kweli ikiwa tutakuwa na kundi kubwa la watu lililokuwa halizalishi kwa kukosa kushughulikiwa ipasavyo au kwa kukosa nyenzo za msingi za kuendesha maisha,” Dk Shein alieleza.Alifafanua kuwa pamoja na jitihada za kuongeza fursa za mikopo lakini pia Serikali inaendeleza jitihada zake za kuhamasisha uwekezaji nchini hatua ambayo itasaidia kuongeza ajira nchini.
5
Wito huo ulitolewa jana na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu wakati wa droo ya 45 ya Promosheni ya Jaymillions, ambayo imemwezesha mmoja wa wateja wa kampuni hiyo kujishindia kitita cha Sh milioni 100.Hata hivyo, mtu huyo alipopigiwa simu na maofisa wa kampuni hiyo mbele ya waandishi wa habari na Msimamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Mrisho Millao simu ya mteja huyo ilikuwa haipatikani.“Tunaelewa zipo sababu zisizoweza kuzuilika ambazo zinaweza kusababisha simu ya mteja isiwe hewani, lakini pia kuna baadhi ya wateja wana utamaduni wa kuzima simu ambao unaweza ukasababisha mteja akose mawasiliano ya muhimu, kama mteja wetu huyu leo ambaye tulitaka kumpa taarifa ya kujishindia kitita chake kupitia promosheni yetu ya Jaymillions” alisema.Alisema kwa mujibu wa taratibu za Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, kutokana na namba hiyo ya ushindi kutopatikana, wataendelea kufanya jitihada za kumtafuta mshindi kwa njia mbalimbali, ikiwemo kupitia matangazo kwenye vyombo vya habari na kuendelea kumpigia mara kwa mara kwa muda wa wiki mbili, kuona kama kuna wakati atakuwa hewani.Promosheni ya Jaymillions iliyoanza katikati ya Januari mwaka huu, ambayo itadumu kwa siku 100, imeleta faraja na itaendelea kuleta faraja na mafanikio kwa wateja wa Vodacom kwa kuweza kujinasua katika hali duni ya maisha na maisha kuwa murua.Hadi kufikia sasa wameshapatikana washindi wawili wa milioni 100, washindi wanne wa Sh milioni 10 kila mmoja na wengine 38 waliojishindia Sh milioni moja kila mmoja.
5
MWENYEKITI wa Halmashauri ya Walei, Parokia ya Kipawa, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Patrick Kiting’ati amevunjika mkono baada ya ajali ya kugonga treni eneo la Vingunguti, jijini humo.Kiting’ati ambaye upekuzi uliofanywa katika gari aliyokuwa akiendesha, ulionesha pia ni Mhandisi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), alipata ajali jana saa 2:00 asubuhi na kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Ilala ya Amana kwa matibabu.Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Reli, Stanley Kulyamo alisema katika taarifa yake kwa gazeti hili jana kuwa Kiting’ati akiwa na gari namba T702 ACH aina ya Toyota Rav4 yenye rangi ya bluu, aliigonga treni kubwa iliyokuwa inatoka Dar es Salaam kwenda mikoa ya Kigoma, Tabora, Mwanza na Mpanda (Katavi).“Treni ilipofika eneo la Vingunguti, iligongwa na gari ndogo iliyokuwa ikiendeshwa na Patrick Kiting’ati mwenye umri kati ya miaka 45 na 50. Gari ilikuwa inatokea barabara ya vumbi ya Karakata kuja Vingunguti, kitambulisho chake kinaonesha ni mhandisi anafanya kazi uwanja wa ndege(JNIA), ila haijafahamika kitengo gani,”alisema.Alisema majeruhi baada ya ajali, alizimia na baadaye Polisi walimfuatilia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Amana na wakati akitoa maelezo kwa shida, alijitambulisha kuwa yeye ni Katekista (kiongozi wa kanisa) wa Kigango cha Relini.Kamanda alisema madaktari waliiambia Polisi kuwa majeruhi huyo, amevunjika mkono wa kushoto. Paroko wa Kipawa, Padri Joseph Mashaka, aliliambia gazeti hili jana kwa simu kuwa ni Kiting’ati alipata ajali ya kugonga treni na ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Walei katika parokia yake na kutokana na ajali hiyo anatibiwa Hospitali ya Amana. “Ni kweli kapata ajali, anatibiwa Hospitali ya Amana.Kwa sasa sipo parokiani nipo nje ya parokia kwa shughuli nyingine lakini tukio ni la kweli,” alisema Padri Mashaka. Awali, katika eneo la tukio, Kulyamo alisema vibaka waliiba kompyuta mpakato ya majeruhi, lakini Polisi walifanikiwa kuipata baada ya vibaka hao kuidondosha chini, walipoona wanakimbizwa na askari.“Nawaomba watu wazingatie sheria na alama zote zinazoongoza usalama wa reli. Mwingine anavuka barabara eneo la reli amefunga vioo mpaka juu na vina giza (tinted), mwingine kaweka ‘earphone’ hasikii hata honi nje,” alisema.
3
['Mshambuliaji wa PSG Neymar jnr hataichezea timu hiyo katika mechi ya ufunguzi dhidi ya Nimes katika ligi ya daraja la kwanza nchini Ufaransa, huku mabingwa hao wa Ufaransa wakidai kwamba mchezaji huyo huenda akaihama klabu hiyo. ', 'Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya PSG Leonardo amesema kuwa mazungumzo ya uhamisho wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 yamepiga hatua kubwa zaidi ya ilivyokuwa hapo awali. ', 'Hatahivyo klabu hiyo haijatoa ruhusa yoyote ya uhamisho, alisema. ', 'Mchezaji huyo ambye ndiye ghali zaidi duniani amehusishwa na uhamisho katika timu yake ya zamani ya Barcelona mbali na uhamisho mwengine wa Real Madrid. ', 'Neymar alijiunga na PSG 2017 wakati klabu hiyo , iliokuwa ikimilikiwa na kampuni ya uwekezaji ya michezo nchini Qatar ilimlipa Neymar kitita cha £200m ili kumwezesha kujiondoa katika kifungu cha sheria cha kandarasi yake. ', 'Mshambuliaji huyo amefunga magoli 34 katika misimu miwili akiwachezea mabingwa hao wa Ufaransa, ijapokuwa majeraha yameathiri vibaya kampeni yake.', 'Mkufunzi wa PSG Thomas Tuchel alisema kwamba Neymar alishiriki katika mazoezi siku ya Jumamosi lakini bapo alikuwa hajapona vizuri']
4
TAASISI ya Mifupa Muhimbili (MOI) imeunda jopo la madaktari na wauguzi saba, kumhudumia Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Yuda Thadeus Ruwai’chi (pichani) aliyefanyiwa upasuaji wa kuondoa damu kwenye ubongo, huku ikifafanua kwa kina tatizo lake. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kiongozi wa jopo hilo, Profesa Joseph Kahamba ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji wa ubongo, uti wa mgongo na mishipa ya fahamu, alisema pamoja na Askofu Ruwai’chi kuendelea kulazwa katika Chumba cha Uangalizi Maalumu (ICU), lakini anaendelea vizuri.“Mpaka leo asubuhi tumemuona anaendelea vizuri, ameamka, anajitambua na kufuata maelekezo anayopewa, pia anazungumza kidogo akiulizwa,” alisema Profesa Kahamba. Alisema jana walitengeneza jopo la madaktari saba, wanaohusika na tiba yake ikiwa ni daktari wa ubongo, wa usingizi, wa magonjwa ya ndani, wataalamu wa chakula na lishe, daktari wa mazoezi tiba na manesi. Profesa Kahamba alisema askofu huyo kwa sasa anahitaji muda wa kutosha ili apumzike, hivyo waumini pamoja na ndugu ni vizuri kumpa nafasi ya kupumzika. “Kwa sasa tungependa tumpe muda wa kupumzika tunashauri ndugu waandae kitabu ambacho watawapatia ndugu na watu wengine watakaokuja kumuona askofu wakija basi waandike humo kumtakia afya njema bila kumuona ili apate nafasi ya kupumzisha ubongo,” alisema. Profesa Kahamba alisema tatizo linalomsumbua Askofu Ruai’chi linajulikana kitaalamu kama ‘Chronic Subdural Haematoma’ ambalo damu inakuwa imevuja kichwani na kusababisha mgandamizo kwenye ubongo.Alisema vitu vinavyoweza kusababisha tatizo hilo havijulikani moja kwa moja, lakini inaweza kusababishwa na kuumia kichwani, shinikizo la damu kubwa linaloweza kusababisha mishipa kupasuka kichwani pamoja na matumizi ya baadhi ya dawa kwa muda mrefu. “Tatizo hili usipopata tiba kwa haraka damu huendelea kuvuja kichwani na uzito wa damu kuzidi unaoendelea kuleta mgandamizo kwenye ubongo na athari kuongezeka hata kuleta kifo mgonjwa anapochelewa kupata huduma,” alisema. Alizitaja dalili za tatizo hilo kuwa ni kichwa kuuma, kizunguzungu, kichefuchefu, upande mmoja wa mwili kukosa nguvu, kushoto au kulia. Askofu Mkuu Ruwai’chi alifikishwa MOI usiku wa Septemba 9, mwaka huu, na baada ya uchunguzi alibainika kuwa anahitaji upasuaji mkubwa wa dharura, uliofanyika usiku huo kwa saa tatu.Alipokelewa MOI akitokea Hospitali ya Rufaa ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro, alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kubainika kuwa anahitaji matibabu zaidi. Viongozi mbalimbali na waumini wa kanisa hilo, walifika MOI kumjulia hali mgonjwa huyo. Rais John Magufuli ni alifika MOI juzi kumuona na kumuombea apone haraka.
3
  NAIROBI, KENYA Mahakama Kuu ya Kenya imesimamisha uendeshaji wa kesi ya ufisadi dhidi ya Naibu Jaji Mkuu, Philomena Mwilu. Hatua hiyo, inafuatia ombi la Mwilu katika mahakama hiyo kuwa asijibu mashtaka ya ulaghai, utumiaji mbaya wa madaraka na kukwepa kulipa kodi, kesi iliyowasilishwa dhidi yake juzi na Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka ya Umma. Alikamatwa Jumanne katika majengo ya Mahakama ya Juu i na kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu ambapo baadaye aliachiliwa huru kwa dhamana. Kupitia wakili wake, Okongo Omogeni, Mwilu ameiambia Mahakama Kuu jana asubuhi kwamba kesi hiyo iliyowasilishwa dhidi yake ina hila na ni njama dhidi yake. Katika ombi lake mahakamani, alikuwa amewashtaki Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, Idara ya Uchunguzi wa Jinai, Mwanasheria Mkuu na Hakimu Mkuu anayeangazia kesi za ufisadi. Mahakama ya Juu sasa imeamua kusitisha kesi ya uhalifu inayomkabili Mwilu kukisubiriwa kuamuliwa masuala ya kikatiba yanayotokana na ombi alilowasilisha. Jaji Chacha Mwita wa Mahakama Kuu ameeleza ombi hilo la Mwilu linazusha masuala makuu. Naibu Jaji Mkuu huyo anakabiliwa na mashtaka kadhaa yakiwemo kutumia vibaya madaraka yake, na kutolipa ushuru. Inadaiwa kuwa jaji huyo alikiuka sheria ya uongozi na maadili kwa kupokea mkopo binafsi wenye thamani ya dola 120,000 kutoka kwa Benki ya Imperial. Mwilu hata hivyo amejitetea kwa kusema mkopo huo ulitokana na makubaliano ya kibiashara. Mahakama hiyo imeamua sasa kuna masuala ya kutathminiwa kikatiba kubaini iwapo makubaliano ya kibiashara baina ya mtu na taasisi ya kibiashara yanaweza kutazamwa kama mashtaka ya uhalifu. Kwa sasa kesi hiyo ya uhalifu imesimamishwa hadi Oktoba 9.
2
JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha linaendelea kumshikilia Mwenyekiti wa Kijiji cha Bangata, wilayani Arumeru, Michael Silamoi kwa tuhuma za kumshambulia hadi kumsababishia kifo mmoja wa wanakijiji wa kijiji hicho.Mbali na Mwenyekiti huyo, wengine wanaoshikiliwa ni askari mgambo wawili wa kijiji hicho waliofahamika kwa majina ya Balozi Andrea na Wariael Obedi pamoja na mkazi mwingine aliyefahamika kama Onesmo Siyoi.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (RCO), Hassani Omary akizungumza na gazeti hili jana alithibitisha Mwenyekiti huyo na wenzake watatu kuendelea kushikiliwa na jeshi hilo kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa tangu kukamatwa kwao Januari 8, mwaka huu.“Ni kweli Mwenyekiti wa kijiji cha Bangata na wenzake watatu tunaendelea kuwashikilia kwa tuhuma za kumpiga hadi kusababisha kifo cha Stalei Samwel (29) kilichotokea Januari 3, na jalada la kesi hiyo tumeshalipeleka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua zaidi za kisheria,” alisema.Mkuu huyo wa Upelelezi wa Mkoa wa Arusha aliongeza kuwa watuhumiwa hao hawawezi kuachiwa kwa dhamana kutokana na kuwa wanatuhumiwa kwa mauaji na kinachosubiriwa ni taratibu zikamilike ili wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma hizo zinazowakabili.Akizungumza na gazeti hili kijijini hapo, baba mzazi wa marehemu huyo, Samwel Lukumay (77), alisema kuwa kijana wake alikamatwa na mwenyekiti huyo akiwa na watuhumiwa hao wanaoshikiliwa na Polisi pamoja na mwenyekiti wa usalama wa kijiji hicho, Nuruel John ambaye alitoroka baadaye.Alisema kuwa kijana wake alifungiwa katika ofisi ya kijiji na kuanza kushambuliwa na watuhumiwa hao na kwamba chanzo cha tukio hilo ni mwanawe kudaiwa kumjeruhi mmoja wa wanakijiji.Alisema viongozi hao walimjeruhi mwanawe sehemu mbalimbali za mwili wake na kufikia kumnyoa nywele zake kwa kutumia panga, hali iliyosababisha hadi ngozi ya kichwa kutoka.Mzee huyo aliongeza kuwa baada ya viongozi hao kuona hali ya kijana wake ni mbaya walimpeleka katika Kituo cha Polisi Baraa wakidai kuwa alikuwa ni mwizi na kwamba alishambuliwa na wananchi wenye hasira kali jambo ambalo polisi walilitilia shaka na kutoa PF3 ili akapatiwe matibabu kutokana na hali yake aliyokuwa ambapo alifariki
3
Mwenyekiti wa Chama hicho Joseph Kidando alisema wamefanikiwa kukusanya tani 800 kutoka tani 300 zilizokusudiwa kukusanywa kutoka kwa wanachama wake.Akizungumza na wanachama wa Chama hicho kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa Chama uliofanyika kwenye ukumbi wa Mision Ndanda mjini hapa alisema hali hiyo imesaidia kukuza pato la Chama.Kidando aliongeza kuwa Chama kimeweza kuendesha biashara ya ununuzi wa korosho kwa mtaji wa mkopo kutoka benki ya CRDB na kufanikiwa kurejesha mkopo huo vizuri, aidha Chama kimeweza kuwalipa wakulima wote waliouzia korosho zao ndani ya Chama kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani, malipo hayo ni yale ya kwanza, ya pili na malipo ya majaliwa ya Sh 225.“Mafanikio haya yanajidhihirisha wazi kupitia taarifa tulizoziweka wazi kwenye mbao zetu za matangazo ambazo zinaonesha wazi juu ya uendeshaji wa Chama chetu ambacho kwa sasa tumekuwa Chama cha nne kati ya vyama 34 vilivyopo wilayani Masasi,” alisema Kidando.Kwa upande wake Ofisa Ushirika Wilaya ya Masasi, Abirahi Mutabazi aliwahimiza watendaji wa chama hicho kuwa na mfumo mzuri wa utunzaji wa kumbukumbu za fedha kwenye vitabu vya fedha.
5
Na Adam Mbwana NAIANGALIA klabu kama Real Madrid ambayo ina jumla ya wafuasi takribani Milioni 194 kwenye mitandao yake ya kijamii ya Facebook, Twitter na Instagram ambao miongoni mwao ni mimi na wewe, na hapo ndipo napata majibu kwanini klabu hiyo ni klabu tajiri zaidi duniani. Nahama jiji la Madrid moja kwa moja hadi jimbo la Catalunya, napiga mahesabu na kisha nagundua kuwa mabingwa mara tano wa Ulaya, klabu ya Barcelona wana jumla ya wafuasi Milioni 204 kwenye mitandao hiyo ya kijamii. Natoka hapo hadi jiji la Turin, London na Manchester ambapo nagundua vilabu mashuhuri duniani kama vile Juventus, Chelsea, Arsenal na Manchester United vina wafuasi lukuki kwenye mitandao yao ya kijamii ambao usisahau kuwa miongoni mwao ni mimi na wewe. Baada ya mizunguko yote hiyo ndipo kichwa changu kikafunguka ni kwanini makampuni mashuhuri ya vifaa vya michezo duniani kama vile Adidas na Nike, yanapigana vikumbo kila kukicha kuwania kuingia mikataba minono na vilabu hivyo. Lakini wakati nakamilisha mjadala wangu nikajiuliza kichwani, Je, jiji la Madrid lina wakazi Milioni 194? Na hata baada ya kufanya uchunguzi nikagundua kuwa jiji hilo kongwe lina wakazi takribani Milioni 6.5 hadi kufikia mwaka jana. Nikaja kukumbuka kuwa hata mimi ambaye ni mfuasi wa Real Madrid kwenye mitandao ya kijamii si mkazi wa jiji la Madrid lakini bado nafahamu kuwa mabingwa hao mara 13 wa Ulaya wamemsajili Eden Hazard kutoka Chelsea, na nilimuona Hazard akipiga dana dana Santiago Bernabeu. Kweli ulimwengu ni mdogo sana! Faida zake Miaka ya 2008, wimbi la mitandao ya kijamii liliigubika dunia kwa kasi ambapo dunia ilibadilika na kuwa kama Kijiji. Mitandao ya kijamii kama vile Facebook na Twitter ilijipatia umaarufu kwa kasi huku ongezeko la simu janja likirahisisha shughuli nzima na kuwafanya watu kubadilishana taarifa kwa uharaka zaidi. Kama ambavyo makampuni ya kibiashara yaliona fursa mpya ya kuwafikia wateja wao, ndivyo ambavyo vilabu vya mpira viligundua njia mpya ya kuwasiliana na mashabiki wao duniani kote. Waswahili husema “watu ni mtaji” na ndio maana sio ajabu kuona kampuni kama Adidas aikisaini mkataba wa kibabe wa miaka 12 na klabu ya Real Madrid wenye thamani ya Dola Bilioni 1.6 ambazo ni sawa na Shilingi za Kitanzania Trilioni 3.7 Adidas wana kiburi cha kulipa pesa zote hizo kwasababu wana uhakika nembo yao itaonekana kwenye runinga kupitia jezi za Real Madrid wakati wa mechi lakini pia watapata fursa ya kutangaza bidhaa zao kwa watu milioni 194 kupitia kurasa za mitandao ya kijami za klabu hiyo. Kwa kifupi ni kwamba uwepo wa mitandao ya kijamii umekuwa ni mkombozi mkubwa kwa vilabu vya soka duniani kwani makampuni makubwa ya kibiashara yamekuwa yakivutiwa kutangaza bidhaa zao kupitia kurasa za vilabu hivyo zenye wafuasi lukuki ambao miongoni mwao ni mimi na wewe, hali inayopelekea kuongezeka kwa mapato kwa kiasi kikubwa. Kwa kulitambua hilo, vilabu vimekuwa vikitumia mamilioni ya pesa kuajiri wataalamu wa masuala ya maudhui (content) ili kutengeneza maudhui bora yenye kuwavutia watumiaji wa mitandao ya kijamii. Hivyo kwa namna yoyote ile, biashara ya maudhui imepamba moto miaka ya hivi karibuni huku kila klabu ikijaribu kujipambanua kwa namna ya kipekee mbele ya macho ya wafuasi wake. Kwetu pakoje? Tutoke barani Ulaya kisha turudi nyumbani kwetu Tanzania ambapo soka ni kama dini au kabila kwa baadhi ya watu. Ripoti ya mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) iliyochapishwa na mtandao wa Reuters Februari 23 mwaka jana inadai kuwa watumiaji wa mtandao (internet) Tanzania wamefikia Milioni 23 huku watumiaji Milioni 19 kati yao wakitumia simu zao za mkononi. Licha ya idadi hiyo kuongezeka kila siku, lakini ni vilabu vichache sana nchini vimeona umuhimu wa kuhamishia nguvu zao kwenye mitandao ya kijamii na hata vilabu hivyo vilivyoanza, bado vinafanya kama ‘fashion’ tu na sio kama inavyotakiwa kufanyika. Unaizungumzia Simba yenye jumla ya wafuasi Milioni 1.2 kwenye mitandao ya Facebook, Twitter na Instagram katika nchi yenye watumiaji milioni 23 wa mtandao. Unaizungumzia Yanga yenye jumla ya wafuasi wasiozidi hata laki tano kwenye mitandao hiyo mitatu niliyotaja wakati kila uchao hujisifu kwa kuwa na mashabiki wengi zaidi nchini. Ni wakongwe hao hao wa soka la Tanzania ambao wameshindwa kuwa hata na tovuti rasmi ambazo zimebeba taarifa zinazohusu klabu zao, na hizo zilizopo bado haivutii ukilinganisha na vilabu kama Real Madrid na vingine vya barani Ulaya. Je, hiyo ni sahihi katika ulimwengu ambao mitandao ya kijamii ni moja ya vichocheo vya mapato katika soka? Maudhui VS Maudhui Bora Miaka ya hivi karibuni, mtandao wa Instagram umejizolea umaarufu nchini Tanzania, ukiwa ndio chanzo kikubwa cha habari za mastaa wa Bongo flava, Bongo Movie na wanasiasa. Baada ya kuona upepo huo wa Instagram, vilabu vingi vya soka na wachezaji wakafungua akaunti zao ili kutopitwa, na ndio maana ni rahisi kuona klabu ya mpira ikiwa na ukurasa wa Instagram na sio Twitter, YouTube au tovuti (website). Kuwa na akaunti ni jambo moja na kuwa na maudhui bora ni jambo jingine. Je, ni kweli vilabu vya mpira vina maudhui ya kuvutia, zaidi ya kuweka taarifa za mechi na matokeo tu? Hapo ndipo linapokuja suala la ubunifu na weredi. Maudhui (content) ni taaluma inayojitegemea na ndio maana makampuni kama Tigo, Vodacom, CRDB, SportPesa na mengine mengi nchini hulipa mamilioni ya pesa kupata wataalamu wa maudhui katika mifumo ya picha na video. Sio ajabu kwa klabu kama Real Madrid kuwekeza kwenye mitandao ya kijamii kwasababu wanawachukulia wafuasi wao kama wateja wao namba moja wa bidhaa zitokanazo na jina lao. Nafikiri vilabu vyetu vya Tanzania vingeingia kwenye mfumo huo wa kuwachukulia mashabiki kama wateja wao namba moja, na wakishakuwa na dhana hiyo, basi itakuwa ni rahisi kwa wao kutengeneza maudhui yenye kuwavutia wafuasi wengi. Kupitia mitandao ya kijamii vilabu vinaweza kuuza jezi zao mpya na bidhaa nyingine kadha wa kadha hivyo kujiongezea kipato. Mitandao ya kijamii sio sehemu ya kuweka matokeo ya mechi tu au kututambia wachezaji wapya waliosajiliwa, lakini pia ni sehemu ambayo kama vilabu vitaitumia vyema basi makampuni ya kibiashara yatamwaga mamilioni ili kutangaza biashara zao. Nafikiri ufike wakati vilabu vya soka nchini viache kuchukulia poa mitandao ya kijamii na kuiendesha kimazoea kama mtu wa kawaida anavyoendesha akaunti yake binafsi. Wanatakiwa kujua kuwa ile ni sehemu ya kuingiza mamilioni ya pesa hivyo waichukulie kwa umakini mkubwa kwa kuajiri wataalamu waliosomea kazi hizo na wenye mikakati madhubuti ya kuongeza idadi ya wafuasi na kuwalisha maudhui yenye hadhi sawa na ukubwa wa vilabu hivyo. Lakini pia vilabu vinatakiwa kukumbuka kuwa mitandao ya kijamii ni maana halisi ya msemo maarufu wa “Nipe Nikupe” Ili uweze kupata wafuasi wengi, ni lazima uwe mbunifu wa kutengeneza maudhui (content) bora yenye kuwavutia watazamaji kufuatilia kurasa zao, na hiyo inahitaji wataalamu waliobobea kwenye masuala hayo na sio kila mtu mwenye uwezo wa kumiliki Smartphone na kupost. Tunachukulia poa Kama kurasa rasmi za Shirikisho zimeshindwa kutaja majina ya wafungaji kwenye mechi ya kirafiki inayoihusisha timu ya Taifa kwa muda muafaka basi hiyo ni dhahiri shahiri kwamba tunaichukulia poa mitandao ya kijamii. Wakati sisi tukichukulia poa, vilabu kama Everton na Sevilla vinakubali kuja Tanzania kwasababu vinajua fika vitaongeza idadi ya wafuasi kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii. Wakati sisi tukichukulia poa, klabu kama Juventus inajua fika kuwa moja ya faida za kumsajili Cristiano Ronaldo ni kupata wafuasi wapya kwenye mitandao yao ya kijamii ambao watahama na Ronaldo. Juventus iliweza kuongeza jumla ya wafuasi Milioni 10 kwenye mitandao yao ya Facebook, Twitter, Instagram na YouTube kutoka Milioni 49.7 hadi Milioni 59.5 ndani ya siku 70 tu tangu Ronaldo ahamie klabuni hapo. Ni muda muafaka sasa wa kuacha ‘kuchukulia poa’ mitandao ya kijamii kwani imeshajipambanua kuwa chanzo madhubuti cha mapato kwa vilabu vya soka duniani.
4
Alitoa ombi hilo jana mjini Songea kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipofanya ziara katika Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) Kituo cha Songea kukagua kazi ya ununuzi wa mahindi akiwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Ruvuma.Alisema wananchi wa Songea wana imani kubwa na serikali, hata hivyo bado wana shida kubwa ya soko kwa ajili ya mazao yao jambo linalowarudisha nyuma kiuchumi licha ya juhudi kubwa wanazofanya mwaka hadi mwaka.Alisema licha ya serikali kupanga bei ya Sh 500 kwa kilo moja, bado bei hiyo inawanufaisha zaidi mawakala wanaotumia nafasi hiyo kwenda mashambani kununua mahindi kwa bei ndogo ya Sh 200 na kuiuzia serikali kwa bei kubwa na kuwaacha wakulima wakipata hasara.Mbali na hilo aliiomba serikali kuangalia upya utaratibu wa kugawa magunia ya kununulia mahindi kwa mawakala, kwani hauwasaidii wakulima kwa vile magunia hayo yanatolewa kwa watu wenye uwezo wa kifedha au wenye majina makubwa na kusababisha kero kubwa kwa wakulima wa mahindi.Gama aliishauri serikali kugawa magunia kwa wakulima badala ya kuwapa mawakala ambao wanatumia nafasi hiyo kuwanyonya wakulima kwa kwenda vijijini kununua mazao ikiwemo mpunga na mazao mengine ya biashara kwa bei ambayo inamkandamiza mkulima.
5
HUKUMU katika kesi ya uhujumu uchumi dhidi ya wafanyabiashara watatu ikiwemo raia wa China, Yang Feng Glan (66) Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajiwa kutolewa Februari 19, 2019.Glan ambaye ni maarufu kama Malkia wa Tembo na wenzake wanakabiliwa na mashitaka ya jinai ya kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo yenye thamani ya Sh bilioni 13, kinyume cha sheria. Wakili wa Serikali, Wankyo Simon alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Huruma Shaidi, kuwa kesi hiyo ilikuwa imekuja kwa ajili ya hukumu na kwamba wako tayari kuisikiliza.Hata hivyo, Hakimu Shaidi alisema kuna baadhi ya vitu ambavyo anamalizia kuviandaa katika hukumu hiyo hivyo aliahirisha kesi hiyo hadi Jumanne Februari 19, mwaka huu atakaposoma hukumu hiyo. Mbali na Glan, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Salvius Matembo na Philemon Manase, ambao wote wanatetewa na mawakili Nehemia Nkoko na Hassan Kiangio.Upande wa mashitaka katika kesi hiyo uliwasilisha mahakamani hapo mashahidi 11 kwa ajili ya kuthibitisha mashitaka hayo na baadaye, mahakama iliwakuta na kesi ya kujibu washitakiwa hao.Mahakama iliwataka washitakiwa kujitetea ambapo walijitetea chini ya kiapo na pande zote za utetezi na mashitaka waliwasilisha maelezo yao ya ama mahakama iwatie washitakiwa hatiani au iwaachie huru.Washitakiwawanadaiwa Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014 kujihusisha na biashara ya nyara za serikali. Wanadaiwa kufanya biashara ya vipande 706 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilogramu 1889 zenye thamani ya Sh bilioni 13 bila ya kuwa na leseni iliyotolewa na Mkurugenzi wa Wanyama Pori.Wanadaiwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014 Glan aliongoza na kufadhili vitendo vya kijinai kwa kukusanya na kusafirisha vipande hivyo bila kibali chochote kutoka Mkurugenzi wa Wanyama Pori.Washitakiwa Salvius na Manase wanadaiwa kuongoza makosa ya uhujumu uchumi kwa kusaidia biashara ya nyara za serikali kwa kukusanya, Kusafirisha na Kuuza Meno ya Tembo kwa nia yakujipatia faida. Ilidai Mei 21, 2014 Sinza Palestina wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, Manase alitoroka chiniya ulinzi wa Polisi D 7847 Koplo Beatus aliyekuwa akimshikilia kwa makosa ya kuhusika na biashara hiyo.
3
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro Premium Lager imezindua shindano la uchoraji nchi nzima linalojulikana kama ‘Jiachie na Kili Canvas Competition 2020’ linalotarajiwa kufanyika Januari 22, Golden Tulip, Dar es Salaaam.Akizungumza jana Dar es Salaam, Meneja wa bia ya Kilimanjaro, Pamela Kikuli, alisema shindano hilo litashirikisha wachoraji kutoka nchi nzima na mshiriki atatakiwa kuja na kazi aliyochora kwenye kitambaa kigumu cha kuchorea kisichozidi sentimita 60 kwa sentimita 50.“Mchoraji anapaswa kutumia vitambulishi vya bia ya Kilimanjaro kumuongoza katika uchoraji. Vitambulishi hivyo ni Mlima Kilimanjaro, Twiga, nyota tano na michoro ya kiafrika iliyo kwenye lebo,” alisema Kikuli Pia alisema kazi zitapitiwa na kuchunjwa na majaji kupata washindi watano ambao watapewa nafasi ya kuchora papo hapo na mshindi atapata nafasi ya kuchora mchoro maalum ambao utatumika kuelekea kilele cha mbio za Kilimanjaro Marathon pamoja na pesa taslimu Sh milioni mbili.“Mashindano yanafanyika kwa ajili ya kutoa fursa kwa wachoraji ili waonyeshe kazi zao kwa jamii, kuibua vipaji vipya pamoja na kuongeza muamko wa tasnia ya uchoraji nchini,” alisema Kikuli.Aidha alisema shindano litafanyika ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na mbio za Kilimanjaro Marathon 2020 ambazo hufanyika kila mwaka mkoani Kilimanjaro. Naye jaji mkuu wa shindano hilo, Nathan Mpangala, aliwaomba wachoraji kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa hiyo ambayo itawatangaza, kumkutanisha na watu mbalimbali, kuwajengea kujiamini na kuwapatia kipato.Mbali mshindi wa kwanza kupata Sh milioni mbili pia washindi wa pili hadi wa tano ataondoka na kifuta jasho cha Sh laki mbili kila mmoja. Pia kazi itakayoshinda itapelekwa kwenye mbio za Kili Marathon ambazo zitafanyika Machi 1, Viwanja vya Ushirika.
4
Mwamuzi wa mechi hiyo Erick Onoka wa Arusha na Kamisaa Omar Juma walifikia uamuzi wa kuahirisha mechi hiyo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kutwa nzima ya jana na kuharibu uwanja.Taarifa hizo zilisema kuwa uwanja ulijaa maji na kwamba mechi isingewezekana kuchezwa na kwa vile leo uwanja huo utatumika katika mechi nyingine ya Ligi Kuu kati ya Stand United na Mtibwa Sugar, hivyo mechi hiyo itachezwa kesho.Mechi hiyo inatarajiwa kuwa ya vuta nikuvute kutokana na timu hizo kuwania kumaliza kwenye nafasi nne za juu katika msimamo wa ligi. Timu hizo zipo kwenye nafasi ya tatu na ya nne kwenye msimamo wa ligi, Simba ikiwa na pointi 29 na Kagera pointi 24.Simba inataka kushinda mechi hiyo si tu kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kumaliza ligi kwenye nafasi za juu, lakini pia ikitaka kulipa kisasi kwa Kagera Sugar kwani katika mechi ya mzunguko wa kwanza iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, wekundu hao wa Msimbazi walilala kwa bao 1-0.Timu hizo zinakutana zote zikiwa zimetoka kupata matokeo mazuri katika mechi zilizopita ambapo Simba iliifunga Ruvu Shooting mabao 3-0 na Kagera Sugar ikiifunga Mtibwa Sugar mabao 2-1.
4
Na WINFRIDA MTOI, DAR ES SALAAM  BAADA ya kupanga kukutana katika mechi ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), timu ya Simba na Azam, kila mmoja ameonekana kuweka mikakati ya kusonga mbele. Michezo ya robo fainali inatarajia kuchezwa mwishoni mwa mwezi ujao na timu zote zimeanza mazoezi. Timu nyingine zilizotinga hatua hiyo ni Yanga itakayokutana na Kagera Sugar, Ndanda dhidi ya Sahare All Stars, Namungo FC itacheza na Alliance FC. Akizungumzia mchezo huo, Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck, alisema itakuwa ni mechi ngumu na mzuri kutokana na uimara wa timu zote mbili. Sven alizungumza hayo kupitia tovuti ya Simba na kukiri kuwa ni mechi ya kisasi kutokana na kuwafunga Azam katika michezo yote msimu huu. “Ninavyoona itakuwa ni mechi ya kisasi na ngumu, ukiangalia Azam ni timu nzuri kama ilivyo Simba japo tuliwafunga katika mechi mbili za ligi, lazima watataka kulipiza kisasi,” alisema Sven. Kwa upande wa Kocha Msaidizi wa Azam FC, Bahati Vivier, alisema watafanya maandalizi mazuri ili kujipanga kuendelea katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo. “Ratiba tumeiona, tumejipanga kufanya mazuri ili tuwatoe Simba na tuone kama tunaweza kuendelea na safari yetu, nina imani tukijiweka vizuri benchi la ufundi, tukaandaa timu ikawa tayari kutafuta ushindi, mechi itakuwa nzuri. “Kwenye Ligi tumekutana mara mbili wakafanikiwa kutufunga, lakini nasema hii sio ligi ni mechi moja inayotaka timu moja itoke, tutafanya mipango tuwatoe ili kulipa kisasi,”alisema Bahati.
4
WAANDISHI WETU TIMU ya Simba na Yanga, zimeshindwa kutamba baada ya kulazimishwa suluhu katika michezo yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa jana katika viwanja tofauti. Simba ilishindwa kuvuna pointi tatu mbele ya  Ndanda, katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Nagwanda Sijaona, Mtwara. Yanga nayo ilishindwa kufurukuta mbele ya Biashara United, baada ya kulazimishwa suluhu Uwanja Karume, Mara. Sare hiyo inaifanya Simba kufikisha pointi 80, baada ya kucheza michezo 33, ikishinda 25, sare tano na kupoteza mitatu. Matokeo hayo yanaifanya Yanga kufikisha pointi 61, ilizovuna baada ya kucheza michezo 33, ikishinda 16, sare 12 na kupoteza nne. Yanga imejiweka pabaya kwani, inaweza kuenguliwa katika nafasi ya pili na washindani wao wa karibu, Azam ambao jana usiku walitarajiwa kuumana na  Singida United ambayo inakamata mkia na tayari imeshuka daraja. Azam ikishinda mchezo huo itafikisha pointi 62. Timu hizo zimeshindwa kutamba ugenini, ikiwa  ikiwa imebaki wiki moja kabla ya kukutana katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho, utakaochezwa Jumapili hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kabla ya timu hizo kuumana, Simba itakuwa na kibarua cha kuikabili Namungo, katika mchezo utakaochezwa Uwanja wa Ruangwa, Lindi, huku Yanga ikiikabili Kagera Sugar. Simba iliuanza mchezo wa jana kwa kumiliki mpira na kucheza pasi nyingi hasa eneo la katikati ya uwanja. Ndanda kwa upande wao, ilianza kuisoma Simba huku ikitumia mipira mirefu kufika katika lango la wapinzani wao. Dakika ya 14, mlinda mlango wa Ndanda, Ally Mustafa alifanya kazi nzuri kuokoa mchomo hatari wa John Bocco. Dakika ya 17, Luis Miquissone alipoteza nafasi ya kuindikia Simba bao, baada ya  kupokea pasi safi ya Bocco, lakini mkwaju wake haukulenga lengo. Dakika ya 29, Mustafa alifanya kazi nyingine nzuri  ya kupangua shuti kali lililopigwa na Miquissone, kabla ya walinzi kuondosha mpira huo ndani ya eneo la hatari. Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa timu hizo kwenda mapumziko zikiwa nguvu sawa. Kipindi cha pili kilianza kwa Ndanda kuingia uwanjani na nguvu zaidi kwa lengo la kusaka bao. Dakika ya 50, Kennedy Juma wa Simba alilimwa kadi ya kadi ya njao, baada ya kumkwatua Omary Mponda wa Ndanda. Dakika  ya 56, mlinda mlango wa Simba, Aishi Manula alifanya kazi ya ziada kupangua michomo miwili iliyopigwa, mmoja ukiwa wa kichwa uliopigwa na Mponda na kiki ya Abdul Hamis. Dakika ya 66, Simba ilifanya mabadiliko, alitoka Pascal Wawa na nafasi yake kuchukuliwa na Erasto Nyoni. Pia dakika ya 69, aliingia Meddie Kagere kuchukua nafasi ya Bocco kabla ya Gerson Fraga kutoka na nafasi yake kuchukuliwa na Mzamiru Yassin dakika ya 72. Kocha wa Ndanda, Abdul Mingange alifanya mabadiliko dakika ya 75, alimtoa Mponda na kumwingiza Omary Ramadhani kabla ya dakika ya 81 kumtoa Vitalisi Mayanga na kumwingiza Hussein Javu. Dakika ya 83, Javu alilimwa kadi ya njano baada ya kumkwatua Jonas Mkude. Dakika ya 90, Ndanda ilifanya mabadiliko aliingia Kassim Mdoe kuchukua nafasi ya Kigi Makassy. Pamoja na mabadiliko ya kila upande dakika 90 zilikamilika kwa suluhu.
4
Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Jakline Woiso alisema juzi kuwa mapato ya benki hiyo yametokana na kuongezeka kwa mikopo iliyotolewa kwa wateja ambayo imeongezeka kufikia Sh bilioni 670.8 Desemba mwaka jana kutoka Sh bilioni 644.19 iliyofikiwa katika robo ya tatu ya mwaka jana.Alisema sehemu kubwa ya mikopo inayotolewa na Benki M inalenga katika sekta ya viwanda na uzalishaji, biashara, ujenzi, mawasiliano pamoja na kilimo. “Pamoja na ongezeko hilo pia tumeweza kuwa na asilimia 2.5 kiwango ambacho kinaashiria umakini mkubwa katika utoaji na udhibiti wa mikopo kulinganisha na kiwango cha asilimia tano katika taasisi nyingi za kifedha hapa nchini,” alisema.Aidha, alisema faida kabla ya kodi imeongezeka kwa asilimia 16 kutoka Sh bilioni 20.10 hadi Sh bilioni 23.27 ikilinganishwa na mwaka 2014. Woiso alisema faida itokanayo na huduma za kibenki pia imeongezeka kufikia Sh bilioni 23.66 mwishoni mwa mwaka jana, ikilinganishwa na shilingi bilioni 17.89 za mwaka 2014.Kuhusu amana, alisema zimeongezeka kwa asilimia 24 kufikia Sh bilioni 726.89 mwishoni mwaka jana. “Amana hizo zinatokana na wateja mbalimbali hususan mashirika binafsi, taasisi za kiserikali pamoja na taasisi za fedha na asasi zisizo za kiserikali,” alisema.Kaimu Ofisa Mtendaji huyo alisema benki yao itaendelea kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wake kwa mwaka huu wakiendelea kuimarisha timu ya wafanyakazi ambao wamekuwa na umuhimu mkubwa wa mafanikio ya Benki M.
5
HADIJA OMARY, LINDI Mahakama ya Wilaya ya Lindi imemuhukumu mkazi wa kata ya Rutamba, Issa Mpanyanje (51) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wa miaka 10. Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa mahakama hiyo, Liliani Rugalabamo, baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka. Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo mshitakiwa alipewa nafasi ya kujitetea ambapo aliiomba mahakama hiyo imuonee huruma kwani ni mkosaji wa mara ya kwanza pia anayo familia akiwemo mke na watoto wanaomtegemea hivyo iwapo atapata adhabu kali itawafanya wakose huduma zake. Hakimu Rugalabamo akitoa adhabu katika kesi hiyo namba 34/2019, kupitia vifungu 130 kifungu kidogo (1) na (2) (e) na 1321 kifungu kidogo Sheria sura ya 16 kama ilivyofanywa marejeo mwaka 2002 alisema amesikia maombi ya pande zote mbili,lakini kutokana na Sheria kumshika mikono, amemuhukumu kwenda jela miaka 30 na atakapomaliza adhabu yake amlipe mlalamikaji fidia ya Sh milioni mbili. Awali ilidaiwa mahakamani hapo na mwanasheria wa Serikali, Rabia Ramadhani kuwa mshitakiwa huku akitambua anachokifanya ni kosa, Aprili 14 mwaka huu maeneo ya mashambani bila huruma alimbaka mlalamikaji na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri. Inadaiwa mshitakiwa alipata mwanya huo baada ya kumshawishi mlalamikaji waende shambani akamsaidie kuvuna karanga na baada ya kufika huko alianza kumtomasa kisha kumbaka huku akimsisitiza kutomwambia mtu yeyote. Hata hivyo kutokana na maumivu makali aliyokuwa akiyaona Mtoto huyo waliporejea Nyumbani alilazimika kukiuka maagizo aliyopewa na kumweleza mama yake ambapo naye alitoa taarifa kituo cha Polisi ambapo alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
3
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao  Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40)  na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele  ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa  kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020  maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam  kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu.
5
Mwandishi Wetu SHIRIKA la Afya Duaniani (WHO), limekubaliana na hoja za Rais Dk. John Magufuli kuhusu mapambano dhidi ya corona ikiwamo suala la ugonjwa huo kuishi kama ilivyo kwa maradhi mengine kama Virusi vya Ukimwi. Mei 3, mwaka huu Rais Magufuli, wakati akihutubia taifa, alisema kuwa uzoefu unaonesha ni kawaida kuwa kila gonjwa jipya linapotokea watu hupata wasiwasi kama ilivyotokea kwa ugonjwa wa Ukimwi lakini hata watu waliobainika kuambukizwa Virusi vya Ukimwi. Akizungumza katika moja ya vikao vyake hivi karibuni, Mkurugenzi wa dharura wa WHO, Dk. Mike Ryan, alionya dhidi ya kujaribu kubashiri ni lini virusi vya corona vitatoweka. Aliongeza kuwa kama chanjo itapatikana, kudhibiti virusi kutahitaji “juhudi kubwa” katika kuvitokomeza. “Ni muhimu kufahamu hili, virusi vinaweza kuwa janga jingine katika jamii zetu na virusi hivi huenda visiishe,” alisema Dk. Ryan alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya video kutoka Geneva. “Virusi vya HIV havijaisha – lakini tumevizoea,”  Dk. Ryan alisema pia kwamba haamini “mtu yeyote anaweza kubashiri ni lini ugonjwa huu utatoweka”. Kwa sasa kuna chanjo zaidi ya 100 zinazofanyiwa utafiti- lakini Dk. Ryan alisema kuna magonjwa mengine, kama vile tetekuwanga, ambayo bado hayajatokomezwa licha ya kuwa kuna chanjo yake. Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk. Tedros Ghebreyesus, alisisistiza kuwa bado inawezekana kudhibiti virusi vya corona, kwa juhudi. “Suluhu liko mikononi mwetu, na ni shughuli ya kila mtu, na sote tunapaswa kuchangia kuzuia janga hili,” alisema. Mtaalamu wa WHO wa majanga, Maria van Kerkhove pia ameuambia mkutano wa waandishi wa habari kuwa jamii inapaswa kuweka akilini kwamba itachukua muda kuondokana na janga hilo. Kauli zao zinakuja huku nchi mbalimbali zikianza kulegeza hatua za kukaa nyumbani na viongozi wanaangalia uwezekano wa lini na ni vipi wanaweza kufungua shughuli za kiuchumi katika nchi zao. Dk. Tedros alionya kuwa hakuna hakikisho juu ya njia za kulegeza hatua za kukaa nyumbani bila kusababisha wimbi jingine la maambukizi. “Nchi nyingi zingependa kuacha hatua tofauti za kukabiliana na virusi. “Lakini pendekezo letu ni kwamba kukapa chanjo kunahitajika bado katika kila nchi kwa kiwango kiwezekanacho,” alisema Dk. Tedros. Aidha, Dk. aliongeza kuwa kuna fikra za ajabu zinazoendelea kwamba sheria ya kukaa nyumbani inasaidia kabisa na kwamba kuondolewa kwake kutakuwa vizuri na kwamba yote yanaweza kusababisha hatari. Takribani watu 313,771 kote duniani wameripotiwa kufa kutokana na virusi vya corona na zaidi ya visa milioni 4.7 vimerekodiwa duniani kote. Upuliziaji dawa Mwishoni mwa wiki Shirika la Afya duniani (WHO) lilionya kuwa kutumia dawa ya kuua viuatilifu barabarani, kama inavyofanywa katika baadhi ya nchi ikiwamo Tanzania, hakuondoi virusi hivyo vipya na badala yake kunahatarisha Afya. Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na WHO ilisema kuwa kupulizia dawa mitaani na usoni hakuwezi kuwa na tija katika kukabiliana virusi vya corona. “Kupulizia dawa usoni, mitaani, sokoni siyo jambo linalofaa kwa kuwa haiui virusi vya COVID-19 au vimelea vingine kwa sababu hiyo inaondoa viuatilifu tu vilivyojificha kwenye uchafu. Hivyo licha ya kukosekana kwa tiba lakini bado dawa ya kunyunyizia kemikali haiwezi kuua virusi vya corona,” ilisema taarifa hiyo ya WHO. Aidha, WHO kupitia taarifa hiyo ilisema kuwa mitaani na maeneo mengine kama sokoni kusichukuliwe kama sehemu iliko “hifadhi ya maambukizi” ya COVID-19, na kuongeza kwamba dawa viini, hata nje, inaweza kuwa “hatari kwa afya ya binadamu,” alisema.  Shirika hilo lilionya kuwa njia hiyo haifai katika hali yoyote ile. Mei 3, mwaka huu Rais Magufuli alieleza kuwa uzoefu unaonesha ni kawaida kuwa kila gonjwa jipya linapotokea watu hupata wasiwasi kama ilivyotokea kwa ugonjwa wa Ukimwi lakini hata watu wanaobainika kuambukizwa Virusi vya Ukimwi wanakwenda kuposa na kuoa. Alisema wakati wa ugonjwa wa surua ilikuwa marufuku hata kwenda kutembelea eneo hilo na imekuwa hivyo hivyo kwa magonjwa kama ukoma na Kifua Kikuu (TB), ebola, zika, hofu zimekuwa zikijengeka lakini matatizo hayo hatimaye yalipatiwa ufumbuzi. Alisema corona kweli ipo lakini isiyumbishe Watanzania katika msimamo na mwelekeo, wasitishwe na aliendelea kutoa wito hasa kwa vijana ambao muda mwingi wanapost watu wakisema wamekufa kwa corona. Licha ya hali hiyo alipiga marufuku suala la upuliziaji dawa kwa ajili ya kuua virusi vya corona huku akiagiza walioamuru suala hilo lifanyike wachunguzwe kwani huenda kulikuwa na ulaji wao.
0
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumchukua mshitakiwa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power (IPTL), Harbinder Sethi kwa ajili ya kukamilisha kuchukua maelezo yake.Wakili wa Takukuru, Leonard Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika. Alidai kuwa wachunguzi kutoka taasisi hiyo ya Takukuru wataenda kumchukua Sethi gerezani kwa ajili ya kwenda kumhoji ofisini kwao.Wakili wa utetezi, Dorah Mallaba alidai kuwa ni lazima wakili wa mshitakiwa Sethi awepo wakati anapochukuliwa maelezo na maofisa hao wa Takukuru. Hata hivyo, upande huo wa utetezi uliutaka upande wa mashitaka kuhakikisha wanakamilisha upelelezi mapema na kwa wakati ili kesi hiyo iweze kuendelea katika hatua inayofuata.Baada ya mawakili hao kueleza hayo, Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 8, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.Mbali na Sethi mshitakiwa mwingine katika kesi hiyo ni mfanyabiashara James Rugemarila ambao kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu, kumghushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha serikali hasara ya dola za Marekani milioni 22.19 na Sh bilioni 309.46.Washitakiwa hao wanadaiwa kuwa Oktoba 18, mwaka 2011 na Machi 19 , mwaka 2014 jijini Dar es Salaam walikula njama katika nchi za Afrika Kusini, Kenya na India ili kutenda kosa.Aidha, inadaiwa katika mashitaka ya kujipatia fedha kwamba kati ya Novemba 28 na 29, mwaka 2011 na Januari 23, mwaka 2014 katika Makao makuu ya Benki ya Stanbic Kinondoni na Benki ya Mkombozi tawi la Mtakatifu Joseph, kwa ulaghai washitakiwa hao walijipatia kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dola za Marekani milioni 22.19 na Sh bilioni 309. 461.37. Washitakiwa wamerudishwa rumande kwa kuwa mashitaka hayo hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.
3
SUNING, CHINA ALIYEKUWA nyota wa klabu ya Chelsea, Ramires, ameanza kufanya vizuri katika klabu yake mpya ya Jiangsu Suning ya nchini China kwa kuipa bao juzi dhidi ya Anzhi Makhachkala. Mchezo huo ulikuwa wa kirafiki, huku Ramires ukiwa ni wa kwanza tangu ajiunge na klabu hiyo katika dirisha dogo la usajili Januari, mwaka huu kwa kitita cha pauni milioni 25 kutoka kwa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu nchini England. Kiungo huyo wa timu ya Taifa ya Brazil aliitumikia klabu ya Chelsea kwa mkataba wa miaka mitano na nusu kabla ya kujiunga na klabu hiyo ya nchini China. “Nimefurahi na mapokezi ya nchini China na nimeanza vizuri kwa kufunga bao katika mchezo wangu wa kwanza, japokuwa ni mchezo wa kirafiki, lakini nitakuwa nimeandika historia. “Ninahitaji kuzoea mazingira, lakini haitakuwa ngumu sana, nitakwenda sawa na kufurahia Ligi ya huku China,” alisema Ramires. Hata hivyo, klabu hiyo ipo mbioni kuinasa saini ya mchezaji wa Shakhtar Donetsk ambaye ni raia wa nchini Brazil, Alex Teixeira, kwa kitita cha pauni milioni 35.
4
KAMPUNI ya simu ya Bharti Airtel imeongeza hisa, zinazomilikiwa na serikali kwenye kampuni hiyo kutokea asilimia 40 hadi 49.Uamuzi huo umekuja kutokana na agizo lililotolewa na Rais John Magufuli, kuitaka kampuni hiyo kujadiliana na serikali kuhusu umiliki wa serikali kwenye kampuni hiyo. Akizungumza na Rais Magufuli, Ikulu Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kampuni ya Bharti Airtel, Sunil Mittal, Ikulu Jijini Dar es Salaam kuhusu maendeleo ya mazungumzo ya umiliki wa hisa za kampuni ya hiyo, alibainisha kuwa kwa sasa kampuni itabakia na hisa 51 kutokea 60.Mittal alimwelezea Rais Magufuli kuwa mazungumzo kati ya kampuni yake na Serikali, yanaendelea vizuri na kuwa Bharti Airtel imeridhishwa na makubaliano yaliyofikiwa katika masuala, yaliyokuwa yakijadiliwa yenye lengo la kuimarisha kampuni ya Airtel. Alisema kwa kuwa mazungumzo hayo yanalenga kuleta manufaa kwa pande zote mbili pamoja na kuboresha huduma za mawasiliano za kampuni hiyo, uongozi wa Bharti Airtel utashirikiana na serikali kutekeleza makubaliano yatakayofikiwa.Kwa upande wake, Rais Magufuli alisema ni hatua nzuri ya kuanzia kwa kampuni hiyo na kuongeza kuwa pamoja na kuongeza hisa za serikali katika umiliki wa Airtel Tanzania, kampuni hiyo imekubali kutoa gawio kwa serikali ya Tanzania baada ya mazungumzo hayo kukamilika hivi karibuni.“Masuala mengine ya kumalizia mazungumzo haya yataendelea leo ili kumalizia, lakini jambo zuri ni kuwa sasa wamekubali kutoa gawio kwa Serikali ambapo kwa muda wa miaka minane hadi kumi tulikuwa hatujapata gawio, kiasi cha asilimia za gawio nacho watajadili leo, kwa hiyo mimi naona huu ni mwanga mzuri wa kwenda mbele kati ya kampuni ya Bharti Airtel na Serikali ya Tanzania pamoja na kampuni zingine,” alisema Rais Magufuli. Kwenye mazungumzo hayo Tanzania inaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi.
3
Promosheni hiyo ijulikananyo kama “ Jiongeze na Mshiko” ni ya kipekee kwani inampatia mteja kujiunga na kushiriki bure kwa kujibu maswali na kujishinda Sh milioni 1 kila wiki na mwisho wa promosheni kujishindia Sh milioni 2.Na ikiwa mteja atapenda kujishindia zawadi kubwa zaidi ataweza kujiunga na ngazi ya Premium kwa kuchajiwa Sh 300 kwa siku na kupata nafasi ya kujishindia Sh milioni 3 kila wiki na mwisho wa promosheni kujishindia Sh milioni 50.Akizungumza wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo, Meneja huduma za ziada wa Airtel, Prisca Tembo, alisema, “promosheni hii inadhihirisha lengo letu la kuwawezesha watanzania kufikia ndoto zao na huku tukiendelea kutoa huduma bora za kibunifu zinazokithi mahitaji yao.Promosheni ya “Jiongeze na Mshiko” itawawezesha watanzania wengi kujishindia mamilioni ya pesa kila wiki na kuwawezesha kupata fedha kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kijamii na kiuchumi pindi watakapoibuka washindi kwa muda wa wote wa miezi minne.Mteja atatakiwa kujibu maswali na kujikusanyia pointi zitakazomwongezea nafasi ya ushindi na kuweza kujishindia zawadi ya pesa taslimia kupitia promosheni hii ya “Jiongeze na Mshiko” natoa mwito kwa watanzania kujiunga na kupata nafasi ya kujishidia pesa taslimu kila wiki.Akizungumzia jinsi ya kujiunga na kushiriki, Ofisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde alisema “wateja wataweza kujinga na promosheni hii bure kwa kutuma ujumbe wenye neno ‘BURE’ kwenda namba 15470, na kisha kuanza kupokea maswali kwenye simu zao na kujibu maswali bure bila gharama yoyote na kujikusanyia pointi.Mteja atakapomaliza kujibu maswali ya bure atapata ujumbe utakaomuuliza kama angependa kujiunga na ngazi ya premier, ili kuwezeshwa kufunguliwa maswali zaidi na kujikusanyia pointi nyingi kwa zawadi zenye thamani kubwa.Aliongeza kwa kusema maswali yatakayoulizwa ni ya kawaida hivyo tunategemea wateja wetu watafurahia kuyajibu na kupata nafasi ya kujishindia Sh milioni 108 ikiwa ni moja ya njia ya kuwazawadia kwa kutumia huduma zetu.Alitoa mwito kwa Tanzania kuwa waangalifu na kuhakiki taarifa zozote wanazopewa kuhusu ushindi kwa kupiga 100, namba ya huduma kwa wateja.
5
Na Amina Omari -TANGA VITAMBULISHO vya wajasiriamali vilivyotolewa na Rais John Magufuli vimesababisha Halmashauri ya Jiji la Tanga kukosa mapato huku vyanzo vyake vya mapato 15 kufutika na hivyo kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo. Hayo yamesemwa jana na Meya wa Jiji la Tanga, Seleboss Mustafa wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha kuwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kila kata. Alisema kuwa jiji hilo lilikuwa na jumla ya vyanzo vya mapato 38 ambavyo vilikuwa vinatarajiwa kuliingiza halmashauri hiyo bajeti ya Sh bilioni 15 lakini ugawaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wasio stahiki imesababisha kasoro hiyo. Alisema kuwa zoezi hilo kwa kiasi kikubwa limekwamishwa na watendaji wa kata na mitaa kwa kushindwa kusimamia kwa ukaribu ugawaji wa vitambulisho hivyo kwa watu wasiostahili. “Kwa hili watendaji  mmechangia kutukwamisha kwani mpaka sasa mapato yetu yamefikia asilimia 65 huku ikiwa bado mwezi mmoja tuu mwaka wa serikali uishe, lakini nyie mmetoa vitambulisho kwa watu ambao hawakustahiki,” alisema. Alisema ukosefu huo wa mapato umesababisha halimashauri hiyo kushindwa kutekeleza shughuli za kijamii kama usafi wa masoko pamoja na marekebisho ya taa za barabarani. “Watendaji wameshindwa kutafsiri nia ya Rais kwani vitambulisho vimetolewa hadi kwa wavuvi pamoja na wafanyabiashara wakubwa wenye maduka sasa wote wamegeuka na kuwa wajasiriamali,”alisema Mustafa. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Ramadhani Possi,  alisema kuwa ufinyu wa bajeti umesababisha miradi mingi ambayo walikuwa wamepanga kuitekeleza kushindwa kutekelezwa kwa wakati . “Kwa sasa tunajipanga kuboresha miundombinu ya shule zetu kwa kujenga madarasa mapya ukarabati ya vyoo pamoja na madawati ambapo tunafanya kila pale tunapopata fedha japo kidogo,”alisema Possi. Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Selemani Zumo aliwataka watendaji wa jiji kuhakikisha wanafanyakazi kwa uwadilifu na kujituma pamoja na kujua mipaka ya kazi zao.
3
Na Ramadhan Hassan, Dodoma Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla amesema kuwa biashara ya usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi haitafanyika kwenye uongozi wake. Akizungumza bungeni leo Mei 24, wakati akihitimisha hotuba ya bajeti yake katika mwaka wa fedha 2019/20 na kujibu hoja mbalimbali zilizotolewa na wabunge ikiwemo suala la usafirishaji wanyamapori hai amesema biashara hiyo ilishafungwa tangu alipochaguliwa kuwa waziri wa wizara hiyo. ”Biashara ya wanyamapori hai haitafanyika nikiwa kama Waziri wa Maliasili na Utalii kwakuwa suala hilo lilishafungwa. “Wizara imeamua kufunga mlango wa biashara hii, hata awe chawa au kunguni, atakayetaka kufuga afuge ili watanzania waende kwenye Zoo yake kuwatazama wanyama hao,” amesema Kingwangalla. Ameongeza kuwa kuhusu suala la vipepeo kusafirishwa kwenda nje ya nchi wananchi ambao walikuwa wamechukuliwa vipepeo vyao ili viakuzwe watarudishiwa fedha zao na serikali. Wakati huo huo Waziri huyo amesema kuwa Rais John Magufuli ameridhia hifadhi tatu mpya kuingizwa katika orodha ya Hifadhi za Taifa. “Hapa nina hati kutoka kwa Rais, ameridhia hifadhi mpya tatu kuingia katika orodha ya hifadhi za taifa,” amesema Kigwangalla Amezitaja hifadhi hizo mpya kuwa ni hifadhi ya Burigi, Chato, hifadhi ya Rumanyika, Karagwe na Ibanda, Kyerwa.
3
Na PATRICIA KIMELEMETA – DAR ES SALAAM BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), limefuta vyuo 26 vilivyokuwa vinatoa masomo ya ufundi, huku vingine 20 vikisimamishiwa programu zisizosajiliwa na baraza hilo. Pia baraza hilo limesimamisha vyuo viwili baada ya kubainika havijasajiliwa. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Kaimu Katibu Mtendaji wa NACTE, Dk. Adolf  Rutayuga, ilisema uamuzi huo umefikiwa baada ya kubaini makosa  mbalimbali, yakiwamo ya kushindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na kutoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa. Ilisema baraza hilo limekuwa likifuatilia vyuo vya ufundi ili kutathmini kama vinafuata viwango vya ubora wa kitaaluma vilivyowekwa kwa kipindi kirefu. “Kama ilivyoelezwa katika sheria za usajili na kanuni za leseni, kutozingatia matakwa yoyoye yaliyowekwa na baraza, ni kosa kisheria. Kanuni zinasema hatua kali zinaweza kuchukuliwa kwa kila kosa. Kulingana na matokeo ya ufuatiliaji uliofanywa na timu maalumu, baraza lina uwezo wa kuchukua hatua dhidi ya taasisi au vyuo vinavyoshindwa kutekeleza kanuni zilizowekwa. “Baada ya kufanya utafiti, tulibaini vyuo 26 vilishindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na baraza katika cheti cha usajili, vyuo 20 vikitoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika na vyuo viwili vikiwa na vituo vya satellite/kampasi ambavyo navyo havijathibitishwa na chombo husika,” ilisema taarifa hiyo. Taarifa hiyo ilisema baraza hilo limechukua hatua mbalimbali kwa vyuo vya ufundi 48.
3
MATOKEO ya Uchaguzi wa Serikali ya Mitaa yaliyotangazwa juzi na Waziri wa Nchi, Ofi si ya Rais (TAMISEMI) Selemani Jafo, yameibua maoni tofauti kutoka vyama vya siasa.Vyama hivyo ni pamoja na Chama cha Wananchi (CUF), ambacho kimewapongeza wanachama wake walioibuka na ushindi katika maeneo mbalimbali.Kingine ni Chama cha ACT-Wazalendo ambacho kupitia kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Joran Bashange kimesema kinasubiri kupewa majina ya washindi hao na maeneo waliyotokea ili kitoe tamko kuhusu hilo, kikidai kuwa matokeo hayo yameghushiwa.Aidha, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia kwa Msemaji wake, Tumaini Makene, kimesema hakiwezi kuzungumzia msimamo wa matokeo hayo, kwa sababu ambazo gazeti hili halikuweza kupatiwa.Akitangaza matokeo ya jumla juzi jijini Dodoma, Jafo alisema uchaguzi huo uliovishirikisha vyama 19, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na ushindi wa asilimia 99.9.Jafo alisema baadhi ya vyama vya upinzani, vikiwamo Chadema, CUF na ACT ambavyo hata hivyo vilitangaza kutoshiriki uchaguzi huo, wagombea wake wa wameibuka na ushindi.Ushindi ambavyo vyama hivyo vimevipata ni nafasi ya wenyeviti wa vijiji, vitongoji, wajumbe kundi la wanawake na wajumbe mchanganyiko, ambao kimsingi unawapa ridhaa ya kuwa viongozi wa wananchi katika maeneo husika.Vikizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jana, vyama hivyo kupitia kwa wasemaji wao, vilisema kiujumla vilishatangaza kutoshiriki uchaguzi huo, na hata matokeo yaliyojitokeza baada ya uchaguzi huo yamewashangaza.Msemaji wa CUF, Abdul Kambaya alisema wanachojua kilichosababisha wagombea wao kuibuka na ushindi huo, ni kutokana na majina yao kutoondolewa katika kwa msimamizi wa uchaguzi, licha ya kuwa waliwaandikia barua ili majina yao yaondolewe baada ya wao kutangaza kujitoa.Alisema mshindi wao wa nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji, Damian Gwimo wa Kijiji cha Kamkubwa Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, aliyepata kura 643 dhidi ya 420 ya mpinzani wake kutoka CCM, ushindi wake umetokana na mapenzi ya chama hicho waliyonayo wananchi, licha ya mwenyewe kutoshiriki.“Kilichotokea hapa licha ya kuwa tulijitoa, jina lake halikuondolewa na hivyo kuwafanya wananchi kulipigia kura, hatutachukua uamuzi wa kumzuia kuendelea na majukumu yake, kwa kuwa amechaguliwa na wananchi, kufanya hivyo ni kuibaka demokrasia,” alisema Kambaya.Alisema si kwamba CUF haikuutambua uchaguzi huo, bali ilichokuwa ikikipinga ni namna mchakato wake ulivyoendeshwa na kusababisha majina ya wagombea wake wengi kuondolea na kuacha majina mengi ya wagombea kutoka CCM.ACT – Wazalendo kupitia kwa Bashange, alisema ushindi huo umewashangaza na kuwa hawakutegemea kushinda wala kushindwa, kwa kuwa walijitoa mapema, kabla ya mchakato wa kupiga kura kufanyika.Alisema yapo maeneo ambayo rafu za wazi zimejitokeza, ikiwamo orodha ya wapiga kura kuonesha majina ya waliokuwa wagombea wake, huku picha iliyobandikwa katika karatasi, ikiwa tofauti na mhusika mwenye jina lake.“Mfano Kata ya Golani kuna mgombea wetu aitwaye Dansan, jina ni lake katika karatasi, lakini picha ya mtu mwingine. Ukiacha hilo huko Liwale wagombea wetu hawakupewa barua za kushiriki uchaguzi baada ya kukutwa ofisi zimefungwa, lakini cha ajabu katika uchaguzi majina yao yalijitokeza,” alidai Bashange.Alisisitiza kuwa kwa sasa hawana tamko rasmi kuhusu ushindi huo, walioupata hadi pale watakapopata taarifa rasmi kutoka Tamisemi, kuwa ni wapi wameshinda na majina ya washindi, ndipo chama kitatoa msimamo wake.Nao Chadema walisema hawawezi kuzungumzia uchaguzi huo, kwa kuwa walishajitoa na kuongeza kuwa wakati wowote chama kinaweza kutoa tamko lake.
3
TANZANIA imepongezwa kutokana na uamuzi wa kuunda mabaraza ya kiswahili ambayo ni Bakita kwa Tanzania Bara na Bakiza kwa Zanzibar ambayo kimsingi yanasaidia katika masuala ya sera ya lugha ya Kiswahili.Pongezi hizo zilitolewa na Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki (EACK) Profesa Kenneth Simala wakati alipokuwa akizungumza katika mkutano kati ya Kamisheni ya Afrika Mashariki na wadau wa Kiswahili kutoka Tanzania Bara na Zanzibar uliofanyika jijini Dar es Salaam.Mkutano huo ulikuwa na lengo la kutafakari namna Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki inaweza kushirikiana na serikali ya Tanzania na wadau kuandaa mafunzo yatakayoweza kuwasaidia Watanzania kukiendeleza kiswahili sio tu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki lakini pia ulimwenguni kote ambako Kiswahili kinatumika.“Kwanza niipongeze Tanzania kwa kuwa na mabaraza ya kiswahili kwa sababu yanasaidia katika sera ya lugha ya Kiswahili, na kuwepo kwa mabaraza haya kumesaidia Kiswahili kuenea nchini Tanzania,” alisema Simala.Alisema baraza la mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki limetoa tamko kuwa kila nchi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inastahili kuwa na baraza la Kiswahili. Kutokana na agizo hilo, nchi zote wanachama zipo katika hatua mbalimbali katika kulifanyia kazi agizo hilo.Aidha, Simala alisema nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki bado hazijakamilisha michakato ya kuwa na mabaraza hayo lakini Kamisheni imefahamishwa kuwa juhudi zinaendelea katika mataifa ya Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi ili kuweza kuwa na mabaraza hayo.“Kwa kweli kuwepo kwa mabaraza ya kiswahili katika nchi wanachama ni jambo ambalo Kamisheni inaamini itasaidia kuwa na maendeleo ya lugha ya kiswahili kwa sababu kuna mambo ambayo yanahitaji ushirikiano baina ya mabaraza ya nchi moja na nyingine,” aliongeza Simala.Alisema lugha ya kiswahili imesaidia kwa kiasi kikubwa kuleta umoja na utulivu nchini Tanzania hivyo ikiwa lugha hiyo itaendelezwa katika mataifa mengine ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuna uwezekano mkubwa kuleta umoja na utangamano katika nchi wanachama kama ilivyo kwa Tanzania.
3
['Kocha aliyetimuliwa na Tottenham Mauricio Pochettino anataka kumrithi Ole Gunnar Solskjaer kama kocha wa Manchester United. (Manchester Evening News)', 'Tottenham wapo tayari kupokea ofa za usajili za chini ya pauni milioni 40 kwa kiungo wa Denmark Christian Eriksen, 27. (Evening Standard)', 'Spurs haina mpango wa kumsajili kiungo Mserbia anayechezea Manchester United Nemanja Matic, 31. (Manchester Evening News)', 'Rais wa Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa) Aleksander Ceferin amesema teknolojia ya usaidizi ya mwamuzi ama VAR ni "uozo" japo "haiwezekani kurudi nyuma". (Mirror)', 'Arsenal wamefanya mawasiliano na kocha wa zamani wa Valencia Marcelino wakati klabu hiyo ikiendelea kusaka kocha mpya wa kudumu. (Goal - in Spanish)', 'Kocha wa Tottenham Jose Mourinho ameacha kumfuatilia kiungo wa Sporting Lisbon Bruno Fernandes, 25, kutokana na kuwa na dau la pauni milioni 85 katika mkataba wake. (Mail)', 'Kocha wa Manchester United Solskjaer amesema anataka klabu hiyo kufanya maamuzi ya haraka katika dirisha la usajili, akiashiria kuwa mwenyekiti mtendaji Ed Woodward hakufanya maamuzi ya haraka mwishoni mwa msimu wa uliopita. (Evening Standard)', "Manchester City wameingia katika kinyang'anyiro cha kutaka kumsajili mshambuliaji wa Inter Milan na Argentina Lautaro Martinez. Barcelona pia wanamtaka mchezaji huyo mwenye miaka 22. (Sky Sports Italia, via Calciomercato - in Italian)", 'Mshambuliaji raia wa Ufaransa Olivier Giroud atafanya mazungumzo magumu na klabu yake ya Chelsea. Mshambuliaji huyo mwenye miaka 33 anataka kuondoka klabuni hapo mwezi Januari. (Evening Standard)', 'Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amefanya maamuzi ya kutofanya usajili wowote mwezi Januari licha ya klabu hiyo kupwaya kwenye safu ya ulinzi. (Independent)', 'Klabu yeyote ya Ligi ya Primia ambayo itataka kumsajili kocha wa zamani wa Liverpool na Newcastle Rafael Benitez italazimika kulipa fidia ya zaidi ya pauni milioni 20 kwa klabu yake ya sasa, Dalian Yifang ya Uchina. (Mail)', 'Tetesi bora za Jumanne ', 'Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uswidi Zlatan Ibrahimovic, 38, anatarajiwa kugoma kurejea katika ligi ya Primia na badala yake kusaini mkataba na klabu yake nyengine ya zamani ya AC Milan. (Telegraph)', 'Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Arsenal inamtaka nahodha wa zamani wa klabu hiyo Mikel Arteta kuchukua mikoba ya kocha aliyetimuliwa Unai Emery. Kwa sasa Arteta ni kocha msaidizi wa Pep Guardiola katika klabu ya Manchester City. (Mirror)', 'Arsenal ipo tayari, ikibidi, kupitia rekodi na kufanyia usaili mpaka wakufunzi 12 ambao watawania nafasi iliyoachwa wazi na Emery aliyetimuliwa juma lililopita. (Mirror)', 'Everton wanatarajiwa kutomfukuza kocha wao Marco Silva kabla ya mchezo na mahasimu wao wa jadi Liverpool hapo kesho Jumatano. (Express)', 'Kocha Manuel Pellegrini amejiongezea muda wa kuifunza klabu ya West Ham baada ya kuifunga Chelsea. Kibarua cha kocha huyo mzoefu pia kipo mashakani kutokana na timu yake kutokuwa na matokeo mazuri. (Mail)', 'Kocha aliyetimuliwa na klabu ya Tottenham hivi karibuni Mauricio Pochettino amefungua milango ya kurejea katika ligi ya Primia akitamba kuwa yupo tayari kuzamia tena kwenye bahari ya ukufunzi. (Fox Sports, via Mirror)', 'Mlinzi wa Tottenham Jan Vertonghen, 32, anaamini Pochettino amekuwa mhanga wa mafanikio yake mwenyewe klabuni hapo na kuwa wachezaji wote wanahisi kusababisha kufutwa kazi kwa kocha huyo raia wa Argentina. (Evening Standard)']
4
Kwa mujibu wa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, miradi mingi utekelezaji wake ulianza mwaka 2016/17 hivyo inaendelea. Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa reli ya Kati kwa kiwango cha standard gauge, kuhuisha Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) hususan kukamilisha malipo ya ununuzi wa ndege nne, miradi ya chuma cha Liganga na Makaa ya Mawe ya Mchuchuma.Mingine ni uanzishwaji/uendelezaji wa kanda maalumu za kiuchumi, mtambo wa kuchakata gesi asilia Lindi, na shamba la kilimo na uzalishaji sukari Mkulazi. Akizungumzia ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda, alisema itahusisha miradi ya uendelezaji wa eneo la viwanda Tamco Kibaha, tathmini ya matumizi ya eneo la kiwanda cha General Tyre Arusha, mradi wa magadi soda Bonde la Engaruka- Arusha.Pia kuimarisha Mfuko wa Taifa wa Maendeleo ya Wajasiriamali (NEDF), uendelezaji wa maeneo ya viwanda vidogo vidogo katika mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kigoma na Mtwara.“Maeneo mengine ni pamoja na kuendeleza viwanda vya ngozi, kupanua mnyororo wa thamani wa pamba hadi nguo na uzalishaji wa madawa na vifaa tiba nchini. “Kwa lengo hili, serikali itaendelea kuhamasisha uwekezaji binafsi hususan katika viwanda vinavyotumia malighafi zinazopatikana kwa wingi nchini ikiwa ni pamoja na viwanda vya kusindika nyama, maziwa, maji, misitu, chokaa, mawe urembo, gypsum na mazao ya vyakula na matunda,” alifafanua Dk Mpango.Alisema serikali itaendelea kuziimarisha taasisi zake ili kuwekeza katika viwanda kwa njia ya ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi. Kuhusu kufungamanisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu, alisema miradi ya eneo hili ni ile inayolenga kuimarisha upatikanaji wa fursa za elimu na mafunzo ya ufundi.Aliitaja kuwa ni kugharamia elimumsingi bila malipo, kupanua ruzuku na mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, ununuzi wa vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu, ukarabatri na upanuzi wa Maktaba ya Mkoa wa Dodoma na ujenzi wa vyuo vitano katika mikoa ya Geita, Simiyu, Njombe, Rukwa na Kagera.Kwa upande wa afya na maendeleo ya jamii, hatua zitaendelezwa za kuboresha hospitali za rufaa na mikoa, kuhakikisha upatikanaji wa dawa, vifaa na vifaa tiba na vitendanishi katika hospitali, vituo vya afya na zahanati.Pia kuongeza udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza, na kudhibiti maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi hususan kwa vijana. Katika miradi ya maji, kutakuwa na upanuzi wa huduma za maji vijijini, kuboresha huduma za maji katika Jiji la Dar es Salaam, mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda Kahama, Nzega, Igunga, Tabora hadi Sikonge.Mingine ni ujenzi, ukarabati na upanuzi wa huduma za maji mijini na vijijini, na kutoa maji mto Ruvuma kwenda Manispaa ya Mtwara- Mikindani. Akizungumzia mazingira wezeshi kwa uendeshaji wa biashara, Dk Mpango alisema serikali itaendelea na azma yake ya kupanua miundombinu ya huduma za kiuchumi kufikia azma yake ya kuboresha mazingira ya kibiashara.Alisema itahusisha miradi inayoendelea ya ukarabati wa miundombinu ya reli, miradi ya barabara na madaraja katika barabara za Kidahwe- Kasulu-Kibondo-Nyakanazi, Manyoni-Tabora-Uvinza, Tabora- Koga Mpanda.Pia ujenzi wa barabara za juu za Tazara na Ubungo Interchange, ujenzi wa Daraja la Salender na miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (awamu ya II, III na IV) jijini Dar es Salaam. Pia imo miradi ya bandari ikijumuisha bandari za Dar es Salaam, Mtwara, Tanga, Bagamoyo, bandari kavu ya Ruvu na bandari za Maziwa Makuu (Victoria, Tanganyika na Nyasa).Kwa upande wa usafiri wa anga, alisema serikali itaendelea na ujenzi wa jengo la abiria (Terminal III) kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma, Tabora na Mwanza, ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege vya Geita, Sumbawanga, Shinyanga, Mtwara, Musoma, Iringa na Songea na ukarabati wa Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
5
NICHUKUE nafasi hii kumshukuru Rais John Magufuli kwa maagizo yake ya kuzihamisha halmashauri mbalimbali za wilaya kwenda katika maeneo yao ya utawala. JPM, Mungu ataendelea kukupatia neema na maisha marefu kwa uamuzi mzuri, wa busara.Kwa takribani miaka minne nimeongoza halmashauri mbili za wilaya zenye mahitaji tofauti ya wananchi, ikiwamo Halmashauri ya Wilaya Musoma ambayo makao makuu yake yalipangwa kuwa eneo la kata ya Murangi, takribani kilomita 56 kutoka Musoma Mjini.Hata hivyo, hapo awali wafanyakazi wote wa halmashauri hii walikuwa wanaishi Musoma Mjini na mara chache walitembelea huko vijijini kutatua matatizo ya wananchi maskini ambao ndio waajiri wao. Hali hii imenisumbua kwa muda mrefu kwani kila nikizunguka na kamati ya usalama ya wilaya tulikuwa tunakutana na migogoro ambayo ilipaswa kutatuliwa na watumishi wa halmashauri ambao hawako huko.Hali hii ilisababisha mimi Mkuu wa Wilaya kila wiki nitembelee vijiji mbalimbali kutatua migogoro ya ardhi na kuhamasisha shughuli za maendeleo. Halmashauri ilikuwa inakwama kuwafikia wananchi kwa sababu ya gharama za uendeshaji zinazoongezeka kutokana na umbali uliopo kati ya halmashauri ilipo na wananchi.Kwa mfano, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ilikuwa katika eneo la Manispaa na ili kufikia kijiji cha mwisho lazima usafiri kilometa 92. Kwa upande mwingine mwananchi ili apate huduma ya Mkurugenzi lazima asafiri kilometa 92 pia. Kwa uamuzi wa halmashauri kuhamia kwenye maeneo yake ya utawala, Rais Magufuli Mungu akubariki sana. Umefuta machozi ya wananchi wanyonge.Uamuzi huu umeleta faida zifuatazo: Mosi, wananchi watapata huduma kwa haraka na imewapunguzia gharama za usafiri. Pili, usimamizi wa shughuli za maendeleo utaongezeka kwani wafanyakazi wa halmashauri watawafikia kwa wakati wananchi na kutembelea miradi ya maendeleo. Tatu, ukusanyaji wa mapato ya serikali hasa mapato ya ndani ya halmashauri utaongezeka.Nne, matumizi ya halmashauri yatapungua kwa sababu posho za madiwani zitapungua pia kwani kwa sasa vikao wanafanyia kwenye maeneo yao ya utawala. Tano, gharama za utengenezaji wa magari na mafuta zitapungua pia kwa kila halmashauri. Sita, malengo ya kugawanywa kwa halmashauri ili kusogeza kuhudumia kwa wananchi yatakuwa yametimizwa.Katika muda wangu wa miaka minne kama Mkuu wa Wilaya, hali ya halmashauri ya Musoma kufanyia kazi katika eneo la manispaa ilinikera sana. Ni kwa hali hiyo, nilianza kuwatafuta wadau ili tuweze kujenga majengo ya ramani rahisi ya kuhamishia halmashauri katika kijiji cha Murangi na mdau wa kwanza alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Sudan Kusini ambaye alinitumia ramani rahisi ya kujenga majengo ya halmashauri.Halikadhalika, Mbunge wa Musoma Vijijini, Sospeter Muhongo na Mkuu wa Mkoawa Mara, Adam Malima, tuliwahi kutengeneza ramani ya majengo ya ofisi yenye ukubwa wa madarasa manne na tukakubaliana tutatengeneza vyumba vya silingibodi ili halmashauri ihamie kwenye eneo lake la utawala. Wakati tunaendelea mchakato huu maagizo ya Rais yakatoka na binafsi nilipatwa machozi ya furaha.Ninapoandika makala haya leo, Halmashauri ya Wilaya Musoma imehamia eneo la Mugango kwa muda, umbali wa kama kilometa 26 kutoka Musoma Mjini. Eneo hili la Mugango lina majengo yaliyokuwa ya kiwanda cha kuchambua pamba (Mugango Ginnery).Tutakapopata fedha tutajenga majengo ya kudumu katika eneo la Murangi lililopo kilometa 56 kutoka Musoma Mjini na pia ni katikati ya eneo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.Kwa maneno mengine tumehamia kwenye eneo la utawala lakini hatujafika kwenye eneo lengwa la makao makuu ya halmashauri. Hali hii ya kusogea angalau kwa kutumia majengo yaliyopatikana ni mafanikio makubwa kwa wananchi tunaowatumikia. Kwa Halmashauri ya Musoma, eneo la Makao Makuu sio tatizo kwa sababu ya jiografia yake kukaa vizuri.Jiografia ya Halmashauri ya Wilaya imejitenga kiasi kwamba eneo lake lipo upande mmoja kuliko maeneo mengine ambayo halmashauri za Wilaya huzunguka Halmashauri za Miji na Manispaa. Kwa baadhi ya Wilaya jiografia hii imeleta changamoto kubwa kwa wananchi kwani ili mwananchi afike makao makuu ya Halmashauri yake kupata huduma analazimika kupita halmashauri ya mji kwanza.Mfano wa hili ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambayo kwa sasa imehamishia makao yake eneo la Kibara. Halmashauri ya Wilaya Bunda imezunguka eneo la Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa upande mmoja na hivyo mwananchi wa kijiji cha Kyandenge au Kata Muguta na Mihingo kwa mfano, ili apate huduma kwenye makao makuu halmashauri yake atatembea zaidi kilomita 100 ili afike Kibara.Hivyo, lazima apande gari kutoka kijijini kwake hadi Bunda Mjini kama kilomita 50-60 na akifika Bunda atapanda tena gari lingine la kumpeleka Kibara, zaidi ya kilometa 60. Mgawanyo huu haujazingatia malengo mahususi ya kuanzishwa kwa halmashauri hizi ambayo ni kusogeza huduma karibu na wananchi. Mfano mwingine ni Halmashaur ya Wilaya Tarime ambayo imezunguka Halmashauri ya Mji wa Tarime.Halmashauri hii hivi sasa makao makuu yake yapo Nyamwaga na imehamia katika eneo lake la Nyamwaga. Hata hivyo, mgawanyo ulivyokaa unaumiza wananchi maskini kwani mwananchi wa Kijiji cha Bumera, kwa mfano, ili afike Makao Makuu ya Halmashauri yake Nyamwaga lazima asafiri kilomita 60-70 na anapitia katika halmashauri ya mji ndipo apande gari tena hadi Nyamwaga. Lengo kama ni kuwahudumia wananchi tuangalie jiografia na mgawanyo wa maeneo husika.Mfano wa tatu ni Halmashauri ya Wilaya Babati. Halmashauri hii imeizunguka Halmashauri ya Mji wa Babati sehemu yoyote itakapoamuliwa makao makuu ya halmashauri ya wilaya kwa mgawanyo wa jiografia iliyopo sasa itamtesa mwananchi wa upande mmoja wa halmashauri na jimbo la Babati vijijini.Kwa mfano mwananchi wa Kijiji cha Moya Mayoka, kata ya Magara ili apate huduma ya halmashari yake lazima asafiri mpaka Babati Mjini na akifika mjini anapanda tena basi hadi Dareda Misheni. Ina maana mwananchi atasafiri zaidi ya kilometa 180 kwenda na kurudi kupata huduma.
3
Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Sam Mapande alisema jana kuwa wamechukua uamuzi huo kwa sababu hawana uhakika kama hao waliochukua fomu TFF ni wanachama halali wa Yanga.“Hao waliochukua fomu TFF sisi hatuna uhakika kama ni wanachama wa Yanga au la, kwa hiyo wanachotakiwa ni kuomba upya, wapitie taratibu zote za kufanyiwa usaili, wakipitishwa waende kwenye uchaguzi,” alisema Mapande.“Kamati yangu tunawasubiri, wana siku mbili kuna kesho (leo) na keshokutwa (kesho), anayependa kugombea aje achukue fomu, afanyiwe usaili awahi uchaguzi Jumamosi,” alisisitiza.Uamuzi huo wa Kamati ya Uchaguzi umekuja wakati tayari baadhi ya wagombea waliochukua fomu zilizokuwa zikitolewa makao makuu ya Yanga Jangwani Dar es Salaam wameshaanza kampeni tangu juzi kwa ajili ya uchaguzi huo utakaofanyika Jumamosi wiki hii ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.Waliochukua fomu TFF ambao watatakiwa kuchukua fomu upya ni Aaron Nyanda na Titus Osoro wanaowania nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Paschal Laizer, Edgar Chibula, Mohammed Mattaka, Mchafu Ahmed Chakoma na Omari Said wanaowania Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.Awali uchaguzi huo wa Yanga ulipangwa kufanyika Juni 25 ukisimamiwa na TFF, hata hivyo ulizuka mvutano mkubwa kwa Yanga kugoma kusimamiwa uchaguzi wake na TFF. Wakati TFF ikiendelea na mchakato wa utoaji wa fomu za Yanga, uongozi wa klabu hiyo nao ulitangaza mchakato wake na kupanga uchaguzi ufanyike Jumamosi wiki hii.Kufuatia mvutano huo, juzi TFF ikakutana na viongozi wa Yanga na kufikia uamuzi wa kuiruhusu Yanga ifanye uchaguzi kwa kujisimamia yenyewe. Hata hivyo kikao hicho kilikubaliana wagombea waliochukua fomu TFF wahusishwe katika mchakato huo kama walivyo wagombea wengine 19 waliochukua fomu makao makuu ya Yanga.
4
NA RAMADHAN HASSAN-DODOMA NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano, Luhaga Mpina, amekitoza faini ya Sh milioni 10  Kiwanda cha Nyama cha Tanzania Meet Compay cha mkoani Dodoma, kwa kosa la kutokuwa na cheti cha mazingira pamoja na mfumo mzuri wa kutolea  majitaka kiwandani hapo. Mpina alichukua uamuzi huo alipokitembelea juzi ambapo alisema faini ya Sh milioni tatu ni kutokana na kiwanda hicho kukosa mfumo mzuri wa kutolea maji taka. Kutokana na hali hiyo, amekipa siku 14 kiwanda hicho kiwe kimelipa faini hiyo. “Ninawapiga faini ya shilingi milioni saba  kutokana  na kutokuwa na cheti cha mazingira na shilingi milioni tatu ni kwa sababu kiwanda hakina mfumo mzuri wa kutolea maji taka ambayo hutumiwa na wananchi kwa ajili ya bustani na hivyo kuhatarisha afya zao,” alisema. Pia Luhaga alimwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda hicho, Leo Akonaay, kuanza utekelezaji wa kutunza mazingira, ikiwa ni pamoja na kutengeneza mfumo wa kutolea maji machafu. Kwa upande wake, Akonaay alisema amepokea maagizo hayo na wako tayari kuyatekeleza kwa muda waliopewa. Aidha, Mkurugenzi huyo alisema kiwanda hicho huchinja ng’ombe 120 kwa siku kwa ajili ya matumizi ya ndani ya nchi, huku wanaosafirishwa kwenda Omani wakiwa ni 30 hadi 50 kwa siku. “Pia huwa tunachinja mbuzi 500 na  kondoo 300 kwa ajili ya kupeleka Oman,” alisema. Akonaay alisema mwaka jana walikuwa na wawekezaji 13 lakini kwa sasa wamebaki wawili kwa sababu ya kupanda kwa gharama za kodi na huduma za usafirishaji. Mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda hicho, Hendson Alikatery, akizungumza kwa niaba ya wenzake, alisema changamoto kubwa waliyonayo ni kutokuwa na mikataba pamoja na kushinda njaa kwa sababu mwajiri wao hatoi chakula kila siku, jambo ambalo linashusha morali yao ya kufanya kazi.
3
MICHUANO ya mabenki kwa mpira wa kikapu (Bankers Basketball League – BBL 2018), imezidi kushika kasi, ambako mwishoni mwa wiki kikosi cha NMB kiliichapa CRDB kwa pointi 52-42.NMB chini ya Kocha Mkuu Evarist Mapunda, ilitawala kwa kiasi kikubwa pambano hilo lililofanyika kwenye Viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, ambako walimaliza nusu ya kwanza ya mtifuano huo wakiwa mbele kwa 26-15.Katika nusu ya pili, kujiamini kulikopitiliza kuliwafanya nyota wa NMB kupunguza kasi, ambako walijikuta wakimaliza nusu hiyo hiyo kwa kipigo cha 27-26, ingawa havikutosha kuwapa CRDB ushindi wa jumla, hivyo NMB kushinda 52-42.Akizungumza baada ya mchezo, Kocha wa NMB, Mapunda aliwapongeza nyota wake kwa upambanaji uliofanikisha kuibuka na ushindi huo na kwamba wamejipanga kuhakikisha wanautwaa ubingwa wa michuano hiyo inayofanyika kila mwaka.“Tumetimiza lengo la kuibuka na ushindi katika mechi dhidi ya CRDB, nawaponeza nyota wangu kwa upambanaji, na sasa tunaelekea kwenye mazoezi kujiandaa na mechi zijazo kulingana na ratiba, ili kufanikisha lengo kuu la kutwaa ubingwa,” alisema Mapunda.Kabla ya NMB kuichachafya CRDB, pambano la awali juzi lilizikutanisha DTB na TADB, ambako kikosi cha DTB kiliibuka na ushindi wa pointi 73-40, ambako washindi waliongoza kwa 40-16 katika nusu ya kwanza, kisha 33-24 katika nusu ya pili.Mbali na mpira wa kikapu, pia NMB iliwafunga timu ya mpira wa miguu ya CRDB kwa magoli 3-0 katika mchezo uliopigwa mapema na kufuatiwa na mpira wa mikono.
4
NA SALMA MPELI NI mwaka wa majaribu kwa mrembo wa Kiganda, Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’. Hivi ndivyo unavyoweza kusema kutokana na  majanga matatu yaliyotikisa maisha ya mlimbwende huyo kwa mwaka huu. Majanga hayo yalianza kumwandama Mei 25, mwaka huu baada ya mumewe wa zamani, Ivan Semwanga maarufu kama Ivan Don, kufariki dunia akiwa nchini Afrika Kusini. Ikiwa hata miezi miwili haijapita tangu kuondokewa na baba wa watoto wake watatu, mama yake mzazi, Halima Hassan, alifariki dunia Julai 20. Baada ya majanga hayo mawili, mtu wa kumtia moyo kwa karibu alitarajiwa kuwa mzazi mwenzake, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, badala ya kuwa hivyo ndipo kidonda cha kuondokewa na mama yake kilivyotoneshwa kabla ya hata miezi miwili kukamilika baada ya juzi Diamond kukiri kuzaa na mwanamitindo Hamisa Mabeto. Mambo haya yote ndiyo yanayofanya mwaka huu kwa mlimbwende huyo kutokuwa mzuri, ingawa kupitia ukurasa wake wa Instagram ameonekana kutaka mashabiki wake kutoendelea kuchukulia kusalitiwa na Diamond kwa mtazamo hasi na badala yake walichukulie suala hilo kwa mtazamo chanya. Hata hivyo, mrembo huyo hakuweka wazi kama baada ya Diamond kukiri kuzaa na Hamisa Mobetto, sasa ataendelea na mahusiano naye ili kuwatunza pamoja watoto wao wawili ama ataachana naye na kuendelea na maisha yake. Zari kupitia mtandao wa Snapchat, amesema Diamond Platnumz amedanganya aliposema kuwa yeye (Zari) alikuwa na habari zote kuhusiana na mimba hiyo. “Kamwe siwezi kujihukumu kwa kosa la mtu mwingine kwani kama ameamua kunidhalilisha, hiyo ni aibu yake mwenyewe lakini mimi naangalia maisha yangu yanasonga na natazamia zaidi katika kujifunza na kwenda mbele. “Siwezi kulia kwa matatizo ya mtu mwingine, kikubwa ni maisha yangu na akaunti zangu benki zipo vizuri na wala sina wasiwasi,” alisema Zari. Kwa upande wake pia msanii Diamond licha ya kwamba amesema yuko tayari kupiga magoti mpaka Afrika Kusini, kumuomba msamaha mzazi mwenzie huyo, bado atakuwa na mtihani wa kupima mambo yatakayomfanya aidha abaki na Zari ama Hamisa. Zari ni nani Zari mwenye umri wa miaka 37, ni mfanyabiashara ambaye anamiliki magari ya kifahari na yenye gharama kubwa kama Lamborghini Gallardo, BMW- 2006, Chrysler-2008, Audi Q7-2010 na Ranger Rover Sports. Ni binti wa Halima Sultan Hassan na Nasur Hassan akiwa na asili ya Kihindi, Somalia, Burundi na Uganda. Babu mzaa mama yake anatoka India, bibi yake anatoka Uganda, babu mzaa baba ni Msomali ambaye mkewe ni Mrundi. Mrembo huyu alizaliwa Septemba 23, mwaka 1980 na amekulia katika Mji wa Jinja nchini Uganda. Alivyokutana na Diamond Uhusiano wa Zari na Diamond ulianza mwanzoni mwa 2015, ambapo Diamond Platnumz alikwenda Afrika Kusini kwenye tuzo za Channel O na kuibuka na tuzo tatu. Shughuli ya utoaji tuzo hizo ilipokamilika, Zari alimwalika Diamond kushiriki katika ‘party’ maarufu ambayo mwanadada huyo huwa anaiandaa kila mwaka nchini Uganda inayoitwa ‘All White Ciroc Party’. Baada ya sherehe hiyo, walifuatana kwenda nchini Rwanda na Burundi ambapo Diamond alikwenda kwa ajili ya kufanya maonyesho yake. Baada ya muda mfupi picha zao zenye ‘harufu’ ya kimapenzi zilianza kusambaa mitandaoni na kuzua gumzo Afrika Mashariki, ambapo mrembo huyo alikuwa akijulikana zaidi na baadaye kuzama kwenye penzi na kufanikiwa kupata watoto wawili, Tiffah na Nillan. Ivan Don afariki Dunia  Mei 25, mwaka huu, Ivan ndipo alipofariki ambapo wakati bado wakiwa na uhusiano walipata watoto watatu, Pinto, Quincy na Didy. Ivan Don alikuwa mfanyabiashara nchini Uganda na Afrika Kusini, alifariki dunia kwa ugonjwa wa shambulio la moyo katika Hospitali ya Steve Biko Academy huko Afrika Kusini. Diamond kuchepuka na Dillish Methews Mbali na Hamisa, wiki iliyopita katika mitandao ya kijamii, pia zilisambaa taarifa kuwa Diamond Platnumz alikuwa visiwani Zanzibar akila bata na mrembo Dillish Methews ambaye ni mshiriki wa shindano la Big Brother Afrika mwaka 2013, taarifa ambazo msanii huyo wa Bongo Fleva amezikanusha. Hamisa Mobetto naye Kwa upande wa mwanamke aliyezaa na Diamond, Hamissa Mabetto, sakata la ujauzito wake kuhusishwa na Diamond lilianza mapema mwaka huu, ingawa wawili hao walificha mpaka mtoto alipozaliwa ndipo picha na video zilipoanza kusambaa. Licha ya kuwa baada ya mtoto kuzaliwa, Hamisa alianza kuweka vitu mtandaoni vilivyoonyesha mtoto huyo ni wa Diamond, msanii huyo alikana mpaka juzi alipovunja ukimya na kukiri kwamba aliyezaliwa ni mtoto wake. Hamisa alizaliwa mwaka 1994 mkoani Mwanza na alianza masuala ya mitindo baada ya kuibuka mshindi wa shindano la Miss Xxxl Back To School Bash mwaka 2010 linaloandaliwa na kipindi cha XXL ya Clouds Fm. Mwaka 2011 Hamisa alishiriki mashindano ya Miss Dar Indian Ocean na alifanikiwa kushika nafasi ya pili, mwaka huo huo alikuwa mshindi wa pili wa Miss Kinondoni na kufanikiwa kuingia kwenye nusu fainali za Miss Tanzania. Mwaka 2012 Hamisa alishiriki kwenye mashindano ya Miss University Afrika na kuingia hatua ya 10 bora. Kutokea hapo Hamisa amekuwa gumzo kwenye tasnia ya mitindo na filamu pamoja na kunogesha video za muziki ‘Video Vixen’ katika video mbalimbali kama My Baby ya Quick Racka My Baby. Mwaka 2014 Hamisa alitokea kwenye cover page ya Pulse Magazine la Nchini Kenya. Hivi sasa Hamisa ni mama wa watoto wawili ambao ni Fantasy na Abdulatif.  
1
MIKOA ya Kusini imetakiwa kutangaza na kuendeleza vivutio vya asili vinavyopatikana kwenye mikoa yao kuvutia watalii wengi na kuziongezea kipato halmashauri za mikoa.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa agizo hilo kwenye hotuba iliyosomwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga jana kwenye maadhimisho ya siku ya Urithi wa Mtanzania Mikindani, Mtwara.Waziri Mkuu Majaliwa amewataka wakazi hao kuendeleza urithi wa utamaduni wa majengo ya kale na maeneo ya kihistoria kwa kuwa ni rasilimali kubwa kutokana na kuwavutia watalii wa ndani na nje ya nchi wanaotembelea maeneo hayo.Alisema hatua hiyo itawaongezea mapato na alizotolea mfano Israel na Misri kuwa ni baadhi ya nchi zisizo na rasilimali ya wanyama pori lakini zinavuna mapato kutokana na utalii huo.“Napenda mtambue unapoongelea utalii katika nchi za Misri, Israel na hata nchi nyingi za ulaya, utalii wao ni maeneo ya Mambo ya Kale, hususani miji, majengo ya kihistoria na makumbusho. Tanzania tumebarakiwa kuwa na vyote, yaani wanyamapori, fukwe za bahari, milima, misitu na mambo ya kale,” amesema.Amesema ni fursa sasa kupitia tamasha hilo la Urithi wa Mtanzania kutangaza vivutio vya ndani na nje ya nchi kwa kuwa matamasha hayo yanatangaza na kuhamasisha jamii kupenda na kuenzi utamaduni wao na kuulinda na kuutumia utamaduni kama fursa ya kukuza utalii na fursa zingine ziendazo sambamba na sekta hiyo.Amesema katika kukuza Utalii wa Utamaduni nchini, Wizara ya Maliasili na Utalii imeanza kuboresha sekta ndogo ya Malikale ambayo ni sehemu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo (2025), Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano kuanzia 2016/2017 – 2020/2021.Amesema tamasha hilo ni moja ya michakato ya serikali ya kubaini na kuendeleza vivutio vipya vya utalii nchini kuongeza watalii na mapato kuongeza watalii nchini mwaka 2015 - 2020 kutoka 1,137,182 (2015) hadi 2,000,000 (2020).Tamasha la Urithi wa Mtanzania lilizinduliwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan mkoani Dodoma ambapo aliagiza kila mkoa kuandaa tamasha la urithi huo kila mwaka.Kamati ya Kitaifa ya Urithi wa Mtanzania ilipanga kufanya matamasha Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na Zanzibar. Dodoma, Dar es Salaam, Zanzibar walishafanya.
3
UWEKEZAJI wa mamilioni ya dola uliokuwa moja ya vipaumbele vya Rais John Magufuli alipoingia madarakani mwaka 2015, umewezesha kuanzishwa kwa miradi mikubwa mitano ya kimkakati iliyowezesha ajira zaidi ya 30,000 kwa Watanzania.Alipohutubia Bunge Novemba 25 mwaka 2015 baada ya kuchaguliwa na kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Tanzania, Rais Magufuli alieleza malengo ya kuifikisha Tanzania katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kupitia sekta ua viwanda ili pia kulinda bidhaa za ndani na kuongeza ajira hasa kwa vijana nchini.Akizungumza na waandishi wa habari juzi, jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio ya Serikali kwa miaka minne ya uongozi wa Rais Magufuli, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Geoffrey Mwambe, alisema miradi ya kimkakati kulingana na sheria na kanuni za uwekezaji zimegawanyika katika uwekezaji wa ndani wa Dola za Marekani 100,000 (TSh 223) na nje Dola 500,000.Alisema nje ya hiyo, kuna uwekezaji mkubwa wa mamilioni ya dola ulioelezwa na Rais Magufuli kuutekeleza kwa kipindi chake na kwa miaka minne, mapinduzi makubwa yaliyotokana na kuhamasisha na kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji nchini.“Uwekezaji wa aina hii viashiria vyake ni pamoja na nchi kuaminika kiuchumi na wawekezaji, imani inayowaondolea hofu ya kupoteza fedha wanazowekeza na namna serikali inavyopambana na rushwa na kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji,” alisema.Mwambe alisema kwa miaka minne, Serikali ya Magufuli kupitia uwekezaji mahiri, imewezesha miradi mikubwa mitano ya mabilioni kuanzishwa kupitia TIC. Miradi hiyo ni wa kuzalisha vigae wa kampuni ya Twyford (KEDA), Chalinze; na kiwanda cha matunda cha Sayona cha kampuni ya Motisun Group kijiji cha Mboga, Chalinze. Mingine ni kiwanda cha kutengeneza sabuni ya unga cha KEDS kilichopo Chalinze; Kiwanda cha Nondo cha Kiluwa group cha Mlandizi, Kibaha na kiwanda cha Goodwill cha kutengeneza vigae (marumaru) cha Mkuranga.Vyote vikiwa mkoani Pwani. Mwambe alisema Twyford kinazalisha mita za mraba za vigae 50,000 kwa mwaka huku asilimia 90 ya malighafi wakitoa nchini na asilimia 10 nje ya nchi.Alisema mradi huu wa Dola za Marekani milioni 56 (Tsh bilioni 130) umeajiri maelfu ya vijana. “Mradi mwingine ni kiwanda cha Sayona cha juisi. Hiki kinazalisha tani 300 za matunda kwa siku na kimeajiri Watanzania zaidi ya 800 wa moja kwa moja na 3,000 wasio wa moja kwa moja.Uwekezaji wake ni Dola za Marekani milioni 55,” alisema. Kwa mujibu wa Mwambe, uwekezaji wa kiwanda cha KEDS wenye thamani ya Dola milioni 11.8 wa kiwanda cha sabuni cha pili kwa ukubwa Afrika umetoa ajira zaidi ya 2000 za moja kwa moja huku maelfu wakipata ajira zisizo za moja kwa moja.Alisema Kilua kinachozalisha tani 10,000 za nondo kwa siku ni moja yab uwekezaji mahiri uliotoa maelfu ya ajira huku Goodwill cha vigae cha thamani ya Dola milioni 53 kikitoa ajira zaidi ya 1,500 za moja kwa moja na zaidi ya 3,000 zisizo za moja kwa moja.
3
BOMBAY, India JITIHADA za ukoaji bado zinaendelea katika Jimbo la Kerala  Kusini  Magharibi mwa nchi hii, baada ya kukumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua ya masika inayoendelea kunyesha eneo hilo. Taarifa zilizopatikana mjini hapa zinaeleza kuwa kwa sasa helikopta za kikosi cha anga na cha wanamaji zinafanya kazi ya kuwakoa wakazi wa eneo hilo ambao wamekwama juu ya mapaa ya nyumba, na  zikiwasambazia misaada ya chakula ambao bado hawajaokolewa. Maofisa wa serikali katika eneo hilo wanaeleza timu za uokoaji zimeelekeza nguvu zaidi katika mji wa Chengannur, ambako inasemekana zaidi ya watu  5,000   wamekwama. Mmoja wa wanasiasa katika eneo hilo, Saji Cherian, alionekana akikibubujikwa na machozi wakati akiomba msaada wa kupelekewa   helikopta. “Tafadhairi tunaomba msaada wa helikopta, Tafadhari nisaidieni watu watakufa. Tafadhari tusaidfieni hakuna suluhisho jingine zaidi ta watu kuokolewa,”alisikika akisema mwanasiasa huyo. Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la Uingereza  BBC, Yogita Limaye, aliyepo katika jimbo hilo la  Kerala, alisema   licha ya serikali kupeleka msaada wa hekopta na boti, pia mitumbwi ya wavuvi inatumika kuwaokoa waliokwama huku mingine ikisaidia kusambaza chakula cha msaada. Alisema   mbali  na misaada hiyo ya binadamu, pia wamiliki wa kampuni za mawasiliano wameamua kutoa huduma hiyo bure  kuwasaidia waliokwama, kuweza kutuma na kupiga simu kuelezea  hali inayowakabili. Alisema  hali imekuwa mbaya zaidi kutokana na  barabara za kuingia katika eneo hilo kujaa matope jambo ambalo limewalazimu wanajeshi kutengeneza njia  na madaraja ya dharura kwa ajili ya kurejesha mawasiliano ya barabara. Maofisa wa Kitengo Cha Dharura katika jimbo hilo walisema zaidi ya familia 200,000 zimekwisha kupewa hifadhi ya muda.
2
Taarifa iliyotolewa na TIC jana, ilisema kituo hicho kimewataka wawekezaji hao kuiangalia Tanzania kama eneo muhimu kwao kufanya uwekezaji katika bara la Afrika kutokana na kuwa na mazingira na sera rafiki ya kufanyia biashara.TIC imebainisha kuwa Tanzania ina wananchi wapatao milioni 48, hivyo kuwa na soko zuri kwa bidhaa zao na pia upatikanaji wa malighafi ni rahisi, kuna nguvu kazi ya kutosha na jambo kubwa ni amani na utulivu wa nchi.VF Corporation iliyoanzishwa mwaka 1899, inaingiza kipato cha dola bilioni 12.3 na inajulikana kimataifa katika kutengeneza viatu na vifaa vyake akiwa na bidhaa zaidi 30, washiriki wa biashara 60,000.Baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa ni mavazi ya jeans, michezo, viatu vya michezo.Kwa sasa VF Corporation inaagiza bidhaa katika kiwanda kimoja hapa nchini na inaangalia uwezekano wa kupanua wigo wa manunuzi katika viwanda vingine nchini.Katika ziara yao, wawekezaji hao wamepitia upya mazingira ya uwekezaji nchini kwa lengo la kuangalia uwezekano wa kuhamasisha viwanda vyao vingine kuangalia Tanzania kama asili ya viwanda vya nguo.
5
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Urambo mkoani Tabora, Adam Malunkwi amesema, Urambo inahitaji mwekezaji ajenge kiwanda cha asali il wafugaji nyuki wapate soko la bidhaa hiyo.Amesema kuna vyama 18 warina asali, vimeandikishwa na vimesajiliwa hivyo warina asali wakiunganishwa na akipatikana mwekezaji wa kununua asali utakuwa ukombozi mkubwa kwa wananchi.“Sisi hapa Urambo tuna jengo kabisa ambalo tulishajenga kwa ajili ya warina asali, wafugaji wa asali, kama tukipata mtu wa uhakika tukampa hilo jengo akaliboresha zaidi halafu akawa anakusanya asali yetu, warina asali wetu wakawa wanajua wanapeleka wapi, wakaiweka pale, wakaisindika, wakaiuza katika hali nzuri inaweza ikatusaidia sana” amesema.Kwa mujibu wa Malunkwi, Urambo pia inahitaji mwekezaji katika sekta ya utalii.Amesema, kwenye eneo la Iyumbu kuna eneo la usimamizi wa wanyamapori (WMA) lenye wanyama wengi wakiwemo tembo, simba na wanyama wengine wanaopatikana kwenye maeneo ya hifadhi. Kwa mujibu wa Malunkwi, eneo hilo lipo kilomita 100 kutoka mjini Urambo hivyo watu waende kutalii.“Eneo hilo lina mchango mkubwa sana. Kwa sababu vile vijiji vinavyopakana kwenye ile sera ya kuhifadhi wanyamapori vile vijiji wanavyopakana wanapata mgao ambao unatumika katika shughuli za wananchi kuhudumia miradi ya wananchi” amesema.“Kila baada ya miezi sita mpaka mwaka kati ya milioi 10 mpaka thelathini wanapata ambazo zinasaidia sasa ama ujenzi wa madarasa au zahanati kutegemea kipaumbele cha kijiji husika” amesema.
5
Akifunga Maadhimisho ya Saba ya Siku ya Mlipakodi jana jijini Dar es Salaam, Dk Bilal alisema TRA inatakiwa kuwachukulia hatua kwani inafahamika kwamba wanaharibu mashine hizo kwa lengo la kukwepa kodi kwa kutoingiza taarifa za kodi pale manunuzi yanapofanyika.Alisema, Serikali itasimamia kikamilifu sheria inayomtaka kila mfanyabiashara mwenye mauzo ya kuanzia Sh milioni 14 kwa mwaka kununua mashine hiyo na kuitumia na akaitaka mamlaka hiyo kuwachukulia hatua wale wote wanaolenga kuhujumu mashine hizo.Alitaka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kutokukaa kimya na kuifanya jamii iamini kwamba wanashirikiana na wafanyabiashara hao wakwepa kodi, hasa pale wananchi wenye mapenzi mema na nchi yao, wanapowapa taarifa kuhusu uharibufu wa mashine hizo na wao hawazifanyii kazi.Dk Bilal alisema kitendo cha wafanyabiashara wasio waaminifu kuwashawishi wale waaminifu kugoma kununua na kutumia mashine hizo ili wasiweke kumbukumbu sahihi na hivyo mamlaka kushindwa kukusanya kodi sahihi, ni kitendo kinachoonesha hawajui mikakati sahihi ya biashara na hawajui kwamba mali bila daftari hupotea bila habari.Mwakilishi wa Sekta Binafsi, Ndibalema Mayanja, imeitaka mamlaka hiyo kuweka vizuri mfumo wa kodi na wafanyakazi wake kufanya kazi kwa timu lakini pia wale ambao wanashiriki katika vitendo vya rushwa yaani si wasafi wanatakiwa kuondoka ili wasiendele kuchafua na kuiharibu sifa ya mamlaka hiyo.
5
VATICAN CITY KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, ametumia hotuba yake ya Krismasi kukemea matukio ya kigaidi na siasa kali Magharibi mwa Afrika, ikiwa ni siku moja baada ya wanamgambo kuwauwa watu 35 nchini Burkina Faso. Akitoa ujumbe wake mjini Vatican hivi jana, Papa Francis alilaani mashambulizi dhidi ya Wakristo barani Afrika na kuwaombea wahanga wa mizozo, majanga ya kimaumbile na maradhi kwenye bara hilo. Papa pia alitoa wito wa kufarijiwa wale wanaoadhibiwa kwa ajili ya imani zao za kidini, hasa wamishionari na waumini waliotekwa na wahanga wa mashambulizi ya makundi ya itikadi kali, hasa nchini Burkina Faso, Mali, Niger na Nigeria. Kauli ya Papa Francis imekuja wakati kukiwa na ripoti kwamba wanamgambo wa itikadi kali nchini Burkina Faso wamewauwa watu 35, wengi wao wanawake, baada ya kushambulia maeneo mawili tofauti kwa wakati mmoja kwenye mji mmoja wa kaskazini mwa nchi hiyo na kambi ya kijeshi. Katika hotuba yake ya Krismasi, mbali na kutaja matukio ya kigaidi barani Afrika, Papa Francis aliwaombea pia wale wanaoteseka kutokana na ghasia, majanga ya kimaumbile au mripuko wa maradhi, na pia wahamiaji wanaojaribu kuvuka bahari kuingia barani Ulaya kusaka maisha bora. “Ni dhuluma ndiyo inayowafanya wavuke majangwa na bahari ambazo huwa makaburi yao,” alisema kwenye ujumbe wake wa “Urbi et Orbi” (Kwa Mji na kwa Ulimwengu) katika makao makuu ya kanisa hilo, Vatican. Mashambulizi ya juzi jumanne nchini Burkina Faso yanatajwa kuwa mashambulizi mabaya kabisa kuwahi kufanywa katika taifa hilo la magharibi mwa Afrika, ambalo limekuwa likishuhudia mashambulizi ya makundi ya kigaidi kwa kipindi kirefu sasa.
2
RAIS John Magufuli ametoa mwito kwa jumuiya ya kimataifa, kuondoa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Zimbabwe.Pia, amempongeza Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa kwa hatua madhubuti za kufanya mageuzi ya kiuchumi katika nchi hiyo, Aidha, amesema Tanzania itaiuzia Zimbabwe tani 700,000 za mahindi kutokana na nchi hiyo kukabiliwa na upungufu wa chakula.Rais Magufuli alisema hayo jana baada ya kufanya mazungumzo rasmi kati yake na Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa yaliyofanyika Ikulu Jijini Harare.Vikwazo vya uchumi Dk Magufuli alimpongeza rais huyo, aliisihi jumuiya za kimataifa kuiondolea Zimbabwe vikwazo vya kiuchumi.Alisema katika kipindi kifupi tangu Rais Mnangagwa aingie madarakani, hali ya uchumi imeanza kuimarika ambapo kwa sasa uchumi wa Zimbabwe unakua kwa wastani wa asilimia 3.5, mwaka ujao unatarajiwa kukua kwa wastani wa asilimia 4.2 na mwaka unaofuata utakuwa kwa wastani wa asilimia 4.4.Kutokana na hali hiyo, alisisitiza kuwa jumuiya ya kimataifa inatakiwa kuondoa vikwazo mbalimbali vilivyowekwa dhidi ya Zimbabwe kwa kuwa vikwazo hivyo, vinawaumiza wananchi wa Zimbabwe, wakiwamo watoto na wanawake.Chakula, ushirikiano Alieleza kuwa katika msimu uliopita, Tanzania ilipata ziada ya chakula ya tani milioni 3.3 baada ya kuvuna tani milioni 16.8, ambapo kati yake mahitaji ya nchi ni tani milioni 13.5. Katika mazungumzo hayo, Magufuli aliikaribisha Zimbabwe kujifunza jinsi Tanzania inavyotoa mafunzo ya kujenga taifa kwa vijana kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Alibainisha kuwa JKT inasaidia vijana kuwa wazalendo wa kweli, kuwa na nidhamu na wakakamavu. Pia alielezea kutofurahishwa kwake na kutofanyika kwa Kamati ya Kudumu ya Pamoja (Joint Permanent Commission – JPC) tangu mwaka 1998, hali iliyosababisha kukosekana kwa msukumo wa kutosha wa kutekeleza maeneo muhimu ya uhusiano yenye kuimarisha uchumi wa pande zote. Hivyo, alitaka mawaziri na wataalamu kufanya kikao cha JPC ndani ya mwezi mmoja. Aidha, Rais Magufuli alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuwa rafiki wa kweli wa Zimbabwe na aliahidi kuwa tayari kupeleka walimu watakaofundisha lugha ya Kiswahili katika shule na vyuo vya Zimbabwe.Alitoa wito kwa wafanyabiashara na wawekezaji wa Tanzania na Zimbabwe, kuongeza biashara kati ya nchi hizo ikilinganishwa na hali ilivyo hivi sasa, ambapo kiwango cha biashara katika nchi hizo ni Sh bilioni 22.578 tu.Rais Magufuli kwa mara nyingine aliwapa pole Rais na wananchi wote wa Zimbabwe, kwa kupoteza watu takribani 400 waliofariki dunia katika mafuriko yaliyosababishwa na kimbunga Idai, kilichoikumba Zimbabwe Machi mwaka huu.Alisema Watanzania wanaungana na ndugu zao Wazimbabwe katika majonzi ya kuondokewa na jamaa zao na wanawaombea kwa Mwenyezi Mungu, aziweke roho zao mahali pema peponi.Kuhusu uhusiano wa Tanzania na Zimbabwe, ulioasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Robert Mugabe, alisema Tanzania inatambua na inathamini uhusiano huo wa kihistoria na kidugu na jukumu lililopo sasa ni kuelekeza nguvu nyingi zaidi katika uhusiano na ushirikiano wa kiuchumi, utakaoziwezesha Tanzania na Zimbabwe kuongeza biashara na uwekezaji.Alisema katika mazungumzo yake ya faragha na Rais Mnangagwa, wamekubaliana kusimamia ipasavyo makubaliano yaliyopo katika Kamati ya Pamoja ya Kudumu (Joint Permanent Commission – JPC) kwa manufaa ya nchi zote mbili.“Ujio wangu hapa Zimbabwe ni kuthibitisha kuwa urafiki wetu bado upo imara na sisi Tanzania tumejipanga kuuimarisha zaidi, tunataka tufanye biashara zaidi na ninyi ndugu zetu wa Zimbabwe ili tukuze uchumi wa nchi zetu na kuongeza kipato cha wananchi wetu,” alisisitiza Dk Magufuli.Kauli ya Mnangagwa Kwa upande wake, Rais Mnangagwa alimshukuru Rais Magufuli kwa utayari wake wa kutoa mahindi kwa ajili ya kusaidia upungufu wa chakula nchini Zimbabwe.Alisisitiza kuwa Wazimbabwe watafurahi kupata chakula kutoka kwa ndugu zao Watanzania. Kuhusu maeneo mengine ya ushirikiano ambayo mawaziri walijadiliana kabla ya mazungumzo hayo, Rais Mnangagwa alisema Zimbabwe ipo tayari kuyatekeleza na kukamilisha maeneo mapya, yatakayokubalika na kutiwa saini makubaliano yake.Baadhi ya maeneo hayo ni pamoja na Zimbabwe kuitumia bandari ya Mtwara katika kusafirisha mizigo yake, kushirikiana katika utalii na usafiri wa anga, kubadilishana utaalamu katika kilimo, mifugo na uvuvi. Baada ya mazungumzo hayo, viongozi hao walikutana na waandishi wa habari na kuwaeleza juu ya yaliyojiri wakati wa mazungumzo.Aidha, akizungumza katika hafla ya kumkaribisha Dk Magufuli nchini humo, Rais Mnangagwa alimshukuru Rais Magufuli kwa kukubali mwaliko wake, na kumthibitishia kuwa yeye na wananchi wa Zimbabwe, wanatambua kuwa Watanzania ni ndugu zao, waliojitolea kwa dhati katika ukombozi wao wakiongozwa na dhamira ya dhati ya Mwalimu Nyerere.Alimshukuru Rais Magufuli kwa kuwa kiongozi wa kwanza katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kutoa msaada wa chakula, dawa na vifaa vya kujihifadhi wakati Zimbabwe ilipokumbwa na mafuriko, yaliyosababishwa na kimbunga Idai Machi 2019.Alisema msaada huo uliwagusa Wazimbabwe wengi na kuwakumbusha umuhimu wa kuchukua tahadhari dhidi ya majanga na mabadiliko ya tabia nchi.Alisisitiza kuwa Zimbabwe itabaki kuwa rafiki na ndugu wa kweli wa Tanzania. Alimhakikishia Rais Magufuli kuwa nchi hiyo ipo tayari kukuza zaidi ushirikiano wa kiuchumi, kwa kuongeza biashara na uwekezaji na kushirikiana katika usafiri wa anga.Alimshukuru Dk Magufuli kwa kumpa mbinu mbalimbali za kiuongozi, ikiwemo kuondoa watumishi hewa, ambao wamekuwa mzigo mkubwa kwa serikali.Aliahidi kudumisha ushirikiano kati ya chama chake ZANU-PF na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Dhifa hiyo ya kitaifa ilihudhuriwa na Makamu wa Rais wa Kwanza wa Zimbabwe, Constantino Chiwenga, mke wa Rais wa Zimbabwe, Amai Auxillia Mnangagwa, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula, viongozi wa ZANU-PF, mawaziri wa Tanzania na Zimbabwe na mtoto wa Baba wa Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makongoro Nyerere.Aidha, Rais Magufuli alimaliza ziara yake nchini Zimbabwe kwa kutembelea na kuweka shada la maua katika eneo la kumbukumbu ya mashujaa wa ukombozi wa Zimbabwe.Dk Magufuli aliwasili jijini Harare nchini humo katika ziara yake ya siku mbili juzi, ambapo alipokewa na mwenyeji wake, Rais Mnangagwa kisha kukagua gwaride rasmi, lililoandaliwa kwa ajili yake na kupigiwa mizinga 21.Katika ziara hiyo, Rais Magufuli aliongozana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mangula, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.
3
MLINDA mlango wa klabu ya Manchester United, David De Gea, ametangaza kuiuza nyumba yake iliyopo jijini Manchester, kwa kitita cha pauni milioni 3.85 ambazo ni zaidi ya Sh bilioni 8 za Tanzania. Tangazo la biashara hiyo ya nyumba imewashtua mashabiki wengi wa Manchester na kuwafanya waamini kuwa kipa huyo anatarajia kuondoka mara baada ya kumalizika kwa msimu huu wa ligi. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, amekuwa akihusishwa kutaka kujiunga na mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid wakati wa uhamisho wa wachezaji kipindi cha kiangazi, hata hivyo klabu hiyo ilianza kumwinda mchezaji huyo tangu Januari mwaka huu. Kipa huyo raia wa nchini Hispania, alijiunga na Manchester United akitokea Atletico Madrid mwaka 2011, lakini anadaiwa kutaka kurudi nyumbani. Nyumba ambayo ameiweka sokoni ina jumla ya vyumba vitano vya kulala, sehemu ya kuogelea (swimming pool), uwanja wa tenisi, sehemu ya Sinema pamoja na vitu vingine vingi. Lakini kipa huyo amekanusha kuwa anataka kuuza nyumba hiyo ili aweze kuondoka Manchester United. “Hakuna mtu ambaye anajua maisha yake ya baadaye, lakini kwa sasa naweza kusema ninafurahia maisha ya hapa Manchester United, ni klabu kubwa duniani yenye wachezaji wenye majina makubwa, pia ninafurahia kucheza soka nchini England. “Sijazungumzia suala lolote juu ya kuondoka katika klabu hii, kikubwa ninachokiangalia ni jinsi gani nitaweza kuisaidia timu hii kufanya vizuri katika michezo mbalimbali na siwezi kusema kama nataka kuondoka kwa sasa,” alisema De Gea.
4
NEW YORK, Marekani TAMASHA la wanamuziki mahiri,  Beyonce na mumewe Jay-Z, limemalizika kwa vurugu baada ya kijana mmoja kuvamia jukwaani wakati mastaa hao wakitumbuiza. Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki mjini Atlanta nchini Marekani wakati vinara hao wakitumbuiza, ambapo ghafla kijana huyo akapanda jukwaani na kuanza kuwavuruga wanenguaji, hali ambayo ilisababisha tafrani. Kwa mujibu wa picha za video zilizokuwa zikirekodi tamasha hilo, zinamwonesha kijana huyo akikatiza jukwaani, baada ya kuchomoka kutoka kwa watazamaji kwa kasi na kujikuta akifukuzwa na wanenguaji. Picha hizo za video zinaonesha kuwa wakati tukio hilo linatokea, baadhi ya wasanii wengine waliokuwa jukwaa la juu walikuwa hawafahamu kinachoendelea, kwani wanaonekana wakiendelea kutumbuiza. Picha nyingine za video zilizorushwa na mashabiki ambao wanahoji walinzi walikuwa wapi wakati huo, zinawaonesha wakiwa wamemdhibiti mvamiaji huyo baada ya kufanikiwa kumtia mikononi. “Siwezi kuamini shabiki anaweza kukatiza jukwaani kama hivi,” aliandika mmoja wa mashabiki kupitia ukurasa wake wa Twitter kabla ya kuhoji mahali walipokuwa walinzi hao.
1
MREMBO na mfanyabiashara wa Uganda, Zari Hassan ‘The Boss Lady’, amejinunulia zawadi ya nyumba nchini Afrika Kusini anakoendesha maisha yake kwa sasa katika kumbukizi ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari ambaye ni mama wa watoto watano, wawili akiwa amezaa na mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini, Nassib Abdul maarufu Diamond Platinumz ameandika maneno ya kumshukuru Mungu kwa kuongeza miaka.Ujumbe huo umepokewa kwa maoni tofauti katika mitandao ya kijamii, huku wengi wakimpongeza mwanamke huyo na kumtakia maisha marefu na yenye furaha. Katika ujumbe wake huo, Zari aliandika: “Asanteni kwa wote ambao mmeniletea zawadi kuelekea Birthday yangu, nimejizawadia mwenyewe nyumba mpya, nashukuru kwa baraka za kuona naongeza mwaka mwingine, sina cha kukulipa Mungu. Asante kwa neema zako”. Miaka 39 iliyopita, Septemba 23, ndiyo siku mwanamama huyo mwenye asili ya Uganda alizaliwa na jana Septemba 22 aliwaalika ndugu, jamaa na marafiki katika sherehe za awali kwa ajili ya kupata chakula na vinywaji nchini humo.
4
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM BENKI ya I&M Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, lakini inang’ara kwa kutoa bidhaa na huduma za kipekee ambazo zinakidhi mahitaji yote ya mteja katika soko. I&M Tanzania ilitambulisha akaunti mpya ya wanawake ya Tunaweza inayotoa suluhisho kwa wanawake wa ngazi zote kuanzia mmoja mmoja, wajasiriamali hadi kikundi au taasisi. Akaunti hiyo inajitofautisha kwa kutoa huduma bila malipo yoyote, haina makato ya kila mwezi na viwango vyake vya riba vinavutia kwenye akiba. Akizungumza leo jijini Dar es Salaa, katika maonyesho hayo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo, alisema kuwa bidhaa hiyo mpya imeunganishwa kwenye mtandao wa benki wa kidijitali ili kuwapa wateja huduma bora na endelevu wakati wowote wanapohitaji. Alisema I&M Tanzania ni sehemu ya I&M Holdings Kenya iliyoanzishwa mwaka 1974 kama kampuni ya huduma za kifedha kabla baadaye kubadilishwa kuwa benki ya biashara. “Mwaka huu inasherehekea miaka kumi ya huduma zetu katika soko la Tanzania. Tunafurahi kuendelea kuhudumia wateja wetu na wateja wapya, pia tunashukuru wateja wetu na washikadau wote walioshiriki katikakuiletea benki mafanikio makubwa kwa kipindi chote cha miaka kumi kwenye soko.” “Tunatoa huduma kadhaa za kifedha ikiwa ni pamoja na akaunti ya akiba, current akaunti kwa madhumuni ya biashara, mikopo ya biashara, huduma za kubadili fedha, uhamishaji fedha kitaifa na kimataifa, huduma za kidijitali ambazo hutoa fursa kwa mteja kupata huduma za benki kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *150*32# au kupitia iClick- huduma ya benki kwa njia ya mtandao inayopatikana bila kikomo kwa saa 24,” alisema Anitha Meneja Masoko na Mawasiliano huyo wa benki hiyo, alisema kuwa pia benki yao wanatoa unafuu na urahisi wa kupata mikopo na huduma nyingine kadhaa ambazo ziliwafanya watu waliotembelea banda lake kwenye maonyesho ya Sabasaba lililopo ukumbi wa Karume, upande wa kulia wa lango la kuingilia kuhamasika na kutaka kujua zaidi kuhusu benki hiyo. “I&M inafungua milango kwa Watanzania wote kwenda kujiunga na benki inayojali mahitaji yao, iliyo tayari kuwapa huduma za kipekee za kifedha kupitia wafanyakazi wake wenye uzoefu zaidi katika kutoa huduma bora kwa wateja. “Mbali na kushiriki katika maonyesho ya Sabasaba, benki hiyo inatoa huduma zake bora kupitia mtandao wa matawi yake yaliyoko maeneo ya Maktaba, Indira Gandhi, Nyerere, Kariakoo, Oysterbay pamoja na mikoani ikiwa ni pamoja na Moshi, Arusha na Mwanza,” alisema Timu ya wafanyakazi wa mauzo na idara ya masoko wa benki hiyo kutoka matawi yake ya Dar es Salaam inayoongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M, Anitha Pallangyo na Ofisa Masoko na Mawasiliano, Debora Mwakyoma wapo kwenye maonyesho hayo ili kuwapa wageni na wale ambao wanataka kuwekeza katika benki inayoaminika na salama ikiwa na huduma za ATM zinazopatikana kwa saa 24.
5
Akizungumza na wakulima na wananchi, Dk Shein alisema karafuu ndio alama ya Zanzibar, hivyo ni wajibu wa wananchi kutunza na kuenzi zao hilo kwa manufaa ya nchi na wananchi wake.Alisema serikali imefanya mabadiliko makubwa ya maendeleo ya zao hilo, ikiwemo kufanya mabadiliko katika Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC).Rais alipongeza shirika kutokana na kwenda sambamba na mabadiliko ya maendeleo, ikiwemo kujenga vituo vya kisasa vyenye hadhi ya zao hilo la karafuu.Kwa mujibu wa rais, serikali imekuwa na mipango maalumu ya kuimarisha karafuu kwa kumpa mkulima asilimia 80 ya bei inayouzwa nje, kuzalisha miche 10,000 kila mwaka na kugawiwa wakulima bure na mpango wa kuilinda karafuu ya Zanzibar.Alisema jitihada hizo za Serikali, zinapaswa kuungwa mkono na wakulima na wananchi kwa kuacha tabia ya kuchanganya karafuu na makonyo, kukaanga na kuanika barabarani.Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazurui alitangaza bei ya karafuu kwa mwaka 2014/2015 ni Sh 14,000 kwa daraja la kwanza, Sh 12,000 daraja na pili na Sh 10,000 kwa daraja la tatu.
5
Alisema hayo juzi mjini hapa wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hizi na kusema kuwa ekari hizo hazijawahi kutumiwa kwa kilimo au ufugaji. “Eneo hilo halitumiki na linafaa kwa kilimo, halijawahi kuguswa kwa ajili ya kilimo na ufugaji,” alisema.Alisema lengo la uwekezaji huo ni kuona mapato ya wilaya yanaongezeka na pia wananchi wanafaidika kwa kutumia fursa nyingi za uwekezaji zilizopo katika wilaya hiyo ikiwemo kilimo, ufugaji nyuki na hata ufugaji wa kuku.Pia Mkuu huyo wa Wilaya alisema wananchi katika vijiji 77 vya Wilaya hiyo wamepatiwa elimu ya ufugaji nyuki na kutakuwa na darasa ambalo litatoa elimu na ushauri kwa wafugaji.“Tumeamua kufuga nyuki kibiashara tutahakikisha mafunzo kwa wafugaji yanakuwa endelevu na yanufaishe wananchi wote,” alisema. Alisema lengo la mpango huo ni kuwezesha wananchi wafuge kitaalamu.Alisema elimu hiyo imekuwa ikitolewa na wataalamu wa halmashauri na wengineo ambapo kumekuwa na mafanikio makubwa kwani wananchi wamejua faida za ufugaji nyuki na hata wameweza kufuga kibiashara na kuweka kuongeza kipato cha familia zao.Alisema sasa wilaya hiyo ina vikundi sita vya ufugaji nyuki vilivyosajiliwa na vingine 95 havijasajiliwa. Aidha alitaka wananchi kuwa rafiki wa mazingira kwa kuacha kukata miti ovyo kwa lengo la kuchoma mkaa na kwa matumizi mengine.“Kama mtu hataki kufuga nyuki basi awe mlinzi mzuri wa mazingira,” alisema.
5
MAREKEBISHO ya Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Sura ya 230 yanayojumuisha mapendekezo ya kuzirasimisha kumbi au vibanda vinavyotumika kuoneshea video na hivyo kuratibiwa na sheria hiyo ya filamu, yamepitishwa rasmi na Bunge.Aidha, marekebisho hayo yameweka masharti kwa mtu au kampuni ya kigeni inayotaka kutumia eneo lolote Tanzania kutengeneza filamu, ikiwemo kuwasilisha nakala ya awali iliyotumika kutengeneza filamu husika.Marekebisho hayo yamepitishwa kupitia Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali 8, namba 3 wa mwaka 2019, unaojumuisha marekebisho ya sheria hiyo ya filamu uliowasilishwa bungeni Dodoma jana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardus Kilangi.Akiwasilisha marekebisho hayo alibainisha kuwa muswada huo unapendekeza marekebisho yaliyolenga kuboresha usimamizi na kuweka ubora wa kumbi za sinema na vibanda vinavyoonesha video. Pia alisema yamelenga kuongeza mapato kupitia maboresho ya usambazaji wa filamu kwa watendaji wa filamu pamoja na kuongeza mapato ya serikali.Profesa Kilangi alieleza kuwa lengo la marekebisho hayo ni kuhakikisha kumbi na vibanda vinavyotumika kuoneshea video vinapaswa kurasimishwa chini ya kifungu cha 10 cha Sheria hiyo.“Sehemu hiyo pia inapendekeza kuongezwa kwa kifungu kipya cha 6A, ambacho kimeweka masharti mapya kuhusu utengenezaji wa filamu nchini, yanayomtaka mtu au kampuni ya kigeni kuwasilisha nakala ya awali iliyotumika kutengeneza filamu husika ili kupata kibali cha kutumia eneo la Tanzania katika kutengenezea filamu hiyo,” alisema Profesa Kilangi.
4
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi amesema kwa sasa ofi si imeweka mikakati ya kutafsiri sheria zote ili zisomeke kwa lugha ya Kiswahili. Aliitoa kauli hiyo jijini hapa jana alipokuwa akitoa ufafanuzi kufuatia swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, F aida Bakari (CCM) aliyehoji kama serikali ina mpango kuhakikisha miswada ya sheria zinazoletwa bungeni inaandikwa kwa lugha ya Kiswahili ili kila Mbunge aweze kuzielewa kwa kuwa wanatofautiana kiwango cha uelewa.“Tunaletewa miswada kwa lugha ya Kiingereza watu wanaweza kujadili wakati hawaelewi lugha hiyo. Je serikali haioni ni muda muafaka lugha ya Kiswahili ikatumika kwenye Mahakama, Bunge na maeneo mengine?” Akijibu swali hilo, Dk Kilangi alisema kuwa ofisi yake imeweka mikakati ya kutafisiri sheria zote ili zisomeke kwa lugha ya Kiswahili licha ya kuwa suala hilo linahitaji rasilimali fedha na watu. “Suala hili linahitaji rasilimali fedha na utaalamu wa kutosha maana sheria ina utaalamu wake kuitafsiri kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili, hivyo tunatakiwa kuwa na walaamu ambao watatafsiri bila kupotosha maana halisi.”
3
Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM BEKI wa Yanga, Lamine Moro amewashusha presha mashabiki wa timu hiyo, baada ya kurejea nchini na kusema amerudi kufanya kazi, akipania kuwaonyesha kazi watani wao wa jadi, Simba. Yanga wanatarajiwa kukipiga na Simba Januari 4, mwaka huu katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Hivi karibuni Lamine aliondoka nchini na kwenda kwao Ghana, akidaiwa kuvunja mkataba na Wanajangwani hao kutokana na kutolipwa mishahara yake ya miezi mitatu. Akizungumza katika mahojiano na kituo cha Azam TV, Lamine alisema amerejea kuungana na wenzake tayari kufanya kazi itakayowapa raha mashabiki wa timu hiyo. “Mashabiki wa Yanga wasiwe na wasiwasi kwani nimerejea nchini kufanya kazi, hivyo nitaungana na wenzangu katika maandalizi ya mechi zinazotukabili mbele yetu,” alisema. Akizungumzia mechi yao dhidi ya Simba, Lamine alisema michezo yote ni sawa ila anaamini watafanya vizuri kutokana na maandalizi watakayofanya. Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Yanga, Hassan Bumbuli, alisema timu yao inatarajia kurejea Dar es Salaam leo ikitokea Kigoma ilikokwenda kucheza mechi mbili za kirafiki. “Baada ya timu kuwasili, wachezaji watapewa mapumziko ya siku moja na baada ya hapo, wataendelea na mazoezi kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam dhidi ya Iringa United, mchezo utakaochezwa Desemba 22, mwaka huu, Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam pamoja na mechi za ligi,” alisema. Juu ya Lamine, alisema kuwa ataungana na wenzake mazoezini baada ya mapumziko waliyopewa.
4
WAWAKILISHI pekee wa Afrika Mashariki katika Ligi ya Mabingwa wa Afrika, Simba SC wamewatanguliza mashushushu nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ili kuwachunguza wapinzani wao AS Vita Club watakayokutana nao Jumamosi katika mchezo wa Kundi D.Simba inaongoza katika kundi lake, inatarajia kuondoka kesho Alhamisi kwenda Kongo tayari kucheza dhidi ya AS Vita iliyopo katika nafasi ya tatu ya msimamo wa kundi hilo.Katika mchezo wa kwanza dhidi ya klabu ya Algeria ya JS Saoura, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi jioni huku AS Vita ikifungwa 2-0 katika mchezo uliofuata dhidi ya Al Alhly ya Misri huko Alexandria.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana kuhusu mikakati yao kuelekea kwenye mchezo ujao Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Crescentius Magori alisema mipango ya maandalizi inaenda vizuri ingawa hawataki kuweka wazi mipango yao kutokana na Wakongo wengi kuishi nchini.Alisema wanaofia mipango na mikakati yao kufichuliwa, lakini alisisitiza kuwa tayari Simba imetuma watu wake `wapelezi’ kuifuatilia AS Vita na kuiandalia Simba sehemu ya kufikia na mambo mengine.“Hadi sasa tumetuma watu kuanza kufanya maandalizi ya awali kuelekea kwenye mchezo wetu na wapinzani wetu ili kuhakikisha mipango yetu ya kuvuna ushindi inaenda sawa, tunajua timu za Kongo zinajua fitina kwenye soka na ndio maana hatuwki mipango yetu yote hadharani, “amesema Magori.Amesema idadi ya kikosi kinachoondoka kuelekea kwenye mchezo huo kitawekwa wazi na kocha wa kikosi hicho Patrick Aussems muda wowote baada ya kufanya mazoezi ya jana ya kujiweka fiti kwa mchezo .Hadi sasa gharama za kusafiri mashabiki kwenda kuishangilia timu hiyo kwenye mchezo huo imeshawekwa wazi tiketi ya ndege kwenda na kurudi kwa Kenya Airways kwa Alhamisi ni dola za Marekani 760 sawa na Sh. 1,748,563 kwa siku ya Ijumaa ni dola 850 sawa na Sh. 1,955,757 wakatoi malazi ni dola 70 sawa na Sh. 161,074 wakati viza ni dola 50, sawa Sh 115,052.
4
KINSHASA, Congo DRC WATU 25 wameuawa katika mashambulizi mawili yanayoaminika kutekelezwa na kundi la waasi la Allied Democratic Forces, ADF, katika Mji  wa Beni,uliopo Mashariki mwa nchi hii. Mwandishi wa Sauti ya Amerika (VOA) aliripoti juzi kuwa  idadi ya waliouawa eneo la Mangolikene, nje kidogo ya mji wa Beni, Kivu kaskazini, imeongezeka na kufikia 20. Mwandishi huyo alisema kuwa watu wengine watano  waliuwawa katika kijiji cha Paida  kilichopo karibu na mji huo wa  Beni. Mwandishi huyo aliyepo mjini Goma alieleza kuwa mashambulizi hayo yalitokea usiku wa kuamkia Ijumaa. Alisema kuwa nyumba kadhaa zilichomwa moto na kuna taarifa kwamba baadhi ya watu wametekwa nyara na kikundi cha watu waliowashambulia. Alisema kuwa raia haoa wanasema kuwa waliowashambulia walikuwa wamevalia sare za kijeshi na walikuwa wanazungumza lugha ya Kilingala. Msemaji wa jeshi katika eneo hilo, Kapteni Mak Hazzukay, alisema kwamba mauaji yametokea baada ya waasi kushambulia kambi ya jeshi. Serikali ya DRC imekuwa ikilaumu kundi la ADF kwa mauaji, wizi wa kitumia nguvu na utekaji nyara, lakini wakati mwingine taarifa kamili hukosekana kuhusu wanaofanya mashambulizi. Kundi la ADF, kutoka Uganda, limeuwa mamia ya watu tangu mwaka 2014. Mashambulizi haya ya sasa yanajiri siku moja baada mgombea wa Urais, Martin Fayulu, mmoja kati ya wagombea wengine wa urais, kuzindua kampeni zake katika mji wa Beni.
2
NA RAMADHAN HASSAN, Dodoma   SERIKALI imekiri kukabiliwa na changamoto kubwa ya msongamano wa wafungwa nchini. Imesema wakati wafungwa waliopo magerezani ni  40,000 uwezo wake ni wafungwa  wasiozidi 30,000 hivyo kuzidiwa na wafungwa 10,000. Hayo yalielezwa  bungeni jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamadi Masauni alipojibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum, Lucy Molel (Chadema). Katika swali lake ,Mbunge huyo alitaka kujua Serikali ina mkakati gani wa kupunguza mahabusu  miundombinu iweze kumudu. Masauni alikiri kuwapo   tatizo la msongamano wa wafungwa ambako waliopo kwa sasa ni 40,000 wakati uwezo ni wafungwa 30,000. Naye Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema)   amehoji Serikali inachukua hatua gani kupunguza msongamano wa wafungwa nchini. Akiuliza swali la nyongeza  bungeni jana, Msigwa alisema kuwa Gereza la Segerea, Dar es Salaam limezidiwa na mahabausu. Alisema gereza hilo  lina uwezo wa kuchukua mahabusu 700, lakini waliopo kwa sasa ni mahabusu na wafungwa  2400. “Ukienda katika magereza yetu kuna msongamano mkubwa   kwa mfano Gereza la Segerea ambalo nililipitia juzi lina uwezo wa kuchukua mahabusu 700 lakini sasa hivi lina mahabusu na wafungwa 2400. “Wanalazimika watu kulala upande mmoja mmoja kwa zamu baada ya muda inapigwa ‘alarm’ kisha mnageukia upande mwingine. “Huu ni ukiukwaji wa haki za binadamu na watoto wengi wapo   chini ya umri wanatakiwa waende shule. “Ni kwa nini Serikali imekuwa ikipeleka wanasheria kutetea kesi za Serikali ambao wamekuwa wakilazimisha wale ambao wanaweza kupata dhamana waende kukaa mahabusu kama ambavyo kesi zetu zilikuwa zina dhamana. “Lakini mawakili wa Serikali wamekuwa wakilazimisha tuende kule tukaongeze msongamano?” aliuliza Msigwa. Akijibu, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William ole Nasha, alisema kuwekwa ndani kwa muda mrefu kwa mahabusu hakumaanishi Serikali haitaki kesi hizo zimalizike haraka. “Sababu za msingi ni sababu ya usalama wao. “Wakienda nje wanaweza wakapata matatizo ikiwamo Serikali kuwalinda pili kuna watuhumiwa wakitoka nje wataenda kuharibu ushahidi,”alisema. Mbunge wa Tarime Mjini Ester Matiko (Chadema) katika swali lake la nyongeza, aliitaka serikali iwaachie kina mama ambao wamefungwa huku wakiwa wanaumwa. “Nimekuwa Segerea Mheshimiwa Spika, kule kuna wamama wamefungwa wanadaiwa mathalani Sh 150,000 lakini amefungwa miezi sita kwa gharama ambazo amezitoa Naibu Waziri zinavuka mpaka Sh 200,000. “Kwa nini Serikali isitumie busara kwa kina mama ambao wengine wana watoto wachanga wanafungwa kwa kesi ya Sh 100,000 mpaka Sh 200,000 na Serikali inatumia gharama kubwa katika gharama za chakul?”alihoji Matiko. Akijibu swali hilo, ole Nasha alisema suala hilo ni la  sheria hivyo kama Mbunge anaona hoja hiyo inamashiko apeleke hoja binafsi bungeni. Akiongezea majibu,Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba, alisema   wahalifu hawawezi kuachwa nje kwa kuogopa magereza kujaa.
3
CHRISTOPHER MSEKENA GUMZO kubwa kwenye ulimwengu wa filamu za Kibongo ni waigizaji wapya Flora Kihombo na Rashid Msigala maarufu kama ‘Watoto wa Kamwene’ kushinda tuzo za Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF 2019) katika vipengele vilivyo wakutanisha na mastaa wakubwa. Mtoto Flora Kihombo, aliyeigiza katika filamu ya Kesho aliibuka kidedea katika kipengele cha Mwigizaji Bora wa Kike mbele ya mastaa Wema Sepetu, Monalisa na Johari. Hali kadharika Rashid Msigala, aliwabwaga mastaa wakubwa kama vile Gabo, Madebe Lidai na Hemed Suleiman katika kipengele cha Miwgizaji Bora wa Kiume kupitia filamu yake ya Kesho. Baada ya matokeo hayo kutangazwa, gumzo likawa uhalali wa watoto hao kutoka Iringa kushinda tuzo hizo mbele ya waigizaji wakubwa wenye uwezo, majina makubwa na filamu nyingi. Wengi wakahoji, hivi kweli Rashid  mwenye filamu moja tu anaweza kuwa bora zaidi ya Gabo ambaye amecheza sinema nyingi na mwaka jana alishinda tuzo hizo kama Mwigizaji Bora wa Kiume. Au mtoto Rashid ni bora kuliko ‘role model’ wake Hemed Suleiman na Madebe Lidai ambao wapo kwenye tasnia kitambo na Afrika Mashariki inawatambua kwa kazi zao. Pia hivi inawezekana vipi mtoto Flora Kihombo akawa bora zaidi kuliko Monalisa aliyetwaa tuzo kibao za Kimataifa au Wema Sepetu aliyeshinda tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike mwaka jana  na amefanya kazi na mastaa wakubwa Afrika akiwamo Van Vicker wa Ghana. Ni ngumu kuamini kuwa Flora ana ubora mkubwa zaidi ya Johari ambaye anaelewa uchungu wa tasnia hii toka kipindi kile cha Kaole akiwa na kina Ray Kigosi na Steven Kanumba. Hoja hizo ndiyo zimefanya watoto hao wanaolelewa katika moja ya kituo cha kulele watoto wanaoishi katika mazingira magumu huko Isimani, Iringa wawe maarufu zaidi. Akizungumza na Swaggaz juzi, Jaji Mkuu wa tuzo za Sinema Zetu, Profesa Martin Mhando, anasema kitu ambacho watu hawakifahamu ni kwamba watu walikuwa hawategemei kama watoto wanaweza kushinda. Ndani ya ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam kila mmoja aliyeingia kwenye tuzo zile alikuja na mshindi wake huku wale watoto wakipewa nafasi ndogo ya ushindi. Ndiyo maana kumekuwa na malalamiko juu ya kuwashindanisha watoto na watu wazima jambo ambalo ni kawaida kufanyika kwenye tuzo nyingi zikiwamo zile kubwa kabisa duniani za Oscars. “Watu wengi walikuwa wanategemea mshindi ni yule atakayekuwa amepigiwa kura nyingi na watazamaji na ili tuzo ziwe za kitasnia kwa vyovyote lazima majaji wawe wenye uzoefu katika tasnia na wanaojua namna ya kujaji filamu, “Kwahiyo asilimia 40  ya alama zote zinatoka kwenye kura za watazamaji lakini asilimia 60 zinatoka kwa majaji wao ndiyo wanajua kiwango gani cha Kimataifa au kiwango cha tasnia, ukimpa mtu wa nje ndiyo akuchagulie mshindi basi utakuwa huwezi kujua kama kile kiwango ni kiwango cha Kimataifa au kiwango cha tasnia, “Ndiyo maana tukaamua kwamba watu wapige kura na zile filamu zitakazofikisha asilimia 40 zinaingia katika kinyang’anyiro cha pili ambapo majaji wanazijadili, kwa hiyo wale watoto walitoka kwenye hiyo 40 wakaingia kwenye hii asilimia 60 na wakaonekana ni washindi,” anasema jaji mkuu Mhando. Kwa hiyo unaweza kuona ni namna gani ‘watoto wa kamwene’ walivyoweza kuwapiga bao mastaa baada ya jopo la majaji kuona filamu ya Kesho ina sifa za kutoa Mwigizaji Bora wa Kiume na Mwigizaji Bora wa Kike.
1
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amegeuka ‘mbogo’ baada ya kubaini kuwa kituo cha kisasa cha mabasi cha Msamvu, Morogoro hakijakabidhiwa kwa Manispaa ya Morogoro kama alivyoagiza Rais John Magufuli.Kituo hicho kilitakiwa kukabidhiwa kwa uongozi wa manispaa hiyo na mfuko wa LAPF. Waziri Jafo alishangazwa na kusikitishwa baada ya kusikia taarifa kutoka kwa Meya wa Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga, kuwa hadi sasa ni zaidi ya miezi minne hawajakabidhiwa stendi hiyo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa soko jipya la kisasa la Manispaa hiyo baada ya Serikali kuu kutoa fedha Sh bilioni 17.6."Nasikia kichefu chefu juu ya jambo hili, Rais aliagiza kwa stendi ya mabasi ya Msamvu irudi Manispaa ya Morogoro, ni nani mwingine mwenye mamlaka anayekwamisha utekelezaji huu? " amehoji Jafo.Waziri Jafo amesema baada ya agizo la Rais kwamba Stendi ya Mabasi Msamvu irudi Manispaa ya Morogoro Mei 6, 2018 hakuhitajiki mjadala, kinachofuata ni hatua za utekelezaji.Meya wa Manispaa ya Morogoro Kihanga alisema halmashauri ya Manispaa haijakabidhiwa stendi hiyo ingawa yamefanyika majadiliano baina ya pande mbili hizo na kujitokeza kwa changamoto ya kiwango kikubwa cha fedha kiasi cha Sh bilioni 19 ambacho Mfuko huo unahitaji ili iweze kukabidhi uendeshaji kwa halmashauri.Mei 6, mwaka huu katika hotuba yake ya uzinduzi wa stendi hiyo, Rais John Magufuli amesema, kutokana na mpango mzuri wa mradi huo na kwa vile serikali imekuwa inatoa fedha za ujenzi wa stendi kama hiyo kwenye halmashauri za wilaya nchini, Serikali imeamua kulichukua deni lote lililokuwa ina daiwa na mfuko wa LAPF na kulipwa na serikali.Katika hotuba hiyo alisema baada ya kukabidhiwa stendi hiyo na LAPF, Manispaa hiyo iweke utaratibu wa kuona kwamba kila mfanyabiashara mdogo anapata nafasi ya kufanya biashara katika kufuata utaratibu huo na si kuwabagua, ikiwa ni pamoja na kuwa ni kitega uchumi cha kuiingizia mapato yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii.
3
TANZANIA imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika kupata ngazi ya tatu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa mifumo bora ya udhibiti wa dawa kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).Kwa hali hiyo, TFDA imeingia miongoni kwa asilimia 30 ya taasisi zote za udhibiti wa dawa duniani na imebakiza ngazi moja ya juu inayotolewa na shirika hilo ili kwenda sambamba na taasisi za USFDA ya Marekani, EMA ya Bara la Ulaya, Health ya Canada na TGA ya Australia ambazo tayari zimefikia ngazi hiyo.Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema hatua iliyofikiwa na TFDA ni ya kujivunia kwa sababu imeliweka taifa kwenye ramani ya dunia, hivyo wanapaswa kuendelea kufanya kazi zaidi ya kulinda afya ya jamii ili kufikia ngazi ya nne.Alisema Mei na Novemba mwaka huu, WHO walifika TFDA na kufanya tathmini ya mwisho inayolenga kupima kama mifumo iliyowekwa, imefikia viwango na baada ya tathmini hiyo imejiridhisha mifumo ya mamlaka hiyo imefikia viwango na itangazwe kuwa moja ya taasisi zilizo na mifumo inayofikia kiwango cha tatu cha umahiri.Alieleza mifumo mbalimbali ya udhibiti iliyowekwa, ambayo pia ilifanyiwa tathmini na WHO ni mifumo ya tathmini na usajili wa dawa, mfumo wa ukaguzi wa viwanda vya dawa ndani na nje ya nchi ili kuhakiki utengenezaji bora wa afya na mfumo wa udhibiti wa dawa zinazoingia na kutoka nje ya nchi kupitia mfumo wa forodha.“Pia walifanya tathmini kwenye mfumo wa ufuatiliaji wa ubora wa dawa kwenye soko, mfumo wa kudhibiti majaribio ya dawa, ufuatiliaji wa usalama na ufanisi wa dawa kwenye soko na kusajili maeneo yanayofanya biashara ya dawa. Maeneo mengine ni utendaji bora wa kazi, uchunguzi wa sampuli kwenye maabara na udhibiti wa matangazo ya dawa,” alisema Ummy.Pia aliongeza kuwa kufikiwa kwa hatua hiyo, kunamaanisha nchi itaendelea kupata dawa zilizo bora, salama na fanisi ikiwa zitathibitishwa na TFDA, na dawa duni na bandia, hazitapata nafasi ya kuwepo kwenye soko. Alisisitiza kuwa TFDA haiwezi kuwepo kila mahali, kudhibiti dawa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu kwa sababu nchi ni kubwa na kwamba kuna mipaka bubu ikiwa ni pamoja na kuzungukwa na nchi jirani ambazo mifumo yao bado inaendelea kujengwa.Alisema ili kufikia malengo ni lazima wananchi ishirikiane na mamlaka hiyo kwa kutoa taarifa wanapobaini watu wanaoingiza dawa kimagendo, kutoa taarifa ya madhara ya dawa wakati wa kutumia na kurudisha dawa duni wanazohisi kuwa za bandia kwenye ofisi za TFDA au vituo vya afya.“Hatua hii iliyofikiwa na TFDA ilete matokeo chanya kwenye jamii ili kutekeleza maagizo ya Rais kwamba inapaswa kufanya kazi kwa kuwezesha biashara kufanyika nchinu ili wafanyabiashara waweze kuingiza dawa haraka bila kuchelewesha kwenye vituo vya forodha,” alisema.
3
KATIKA jitihada ya kukwepa panga la Rais John Magufuli chini ya saa 24, Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa limemtia nguvuni Mkandarasi ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Ujenzi ya Fally Enterprises, Felix Lyowa anayedaiwa kuhujumu miradi ya maji yenye thamani ya Sh bilioni 20 .Kati ya miradi hiyo upo mradi wa maji wenye thmani ya zaidi ya Sh bilioni 1.7 uliopo katika mji mdogo wa Laela ambapo ujenzi wake ulikamilika miaka mitatu iliyopita huku ukiwa haufanyi kazi na wananchi kuendelea kuteseka kwa kero ya upatikanaji wa maji .Rais John Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara juzi katika mji mdogo wa Laela kabla ya kuzindua barabara kuu ya Sumbawanga – Laela – Tunduma alimwagiza Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, Mathias Nyange kumkamata Mkandarasi Fally haraka iwezekanavyo . Alimuonya RPC Nyange kuwa akishindwa kutekeleza agizo lake ‘kibarua ‘ chake kitakuwa kimeingia mchanga.Pia alimwagiza yeye (RPC) na Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhakikisha watuhumiwa wote wanaotuhumiwa kuhusika katika kuteketeza kwa moto vifaa 170 vya mionzi ya jua vilivyofungwa katika mradi wa maji Laela wakamatwe na kufikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo.Aidha alimwagiza Waziri wa Maji na Umwagiliaji , Profesa Makame Mbarawa kuwachukulia hatua kali maofisa wa wizara yake walihusika kupatia zabuni nyingi kiasi hicho mkandarasi huyo kinyumbe cha Sheria.Mbali ya Wizara ya Maji pia alimuagiza Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa ,Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru)Mkoa na Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali mkoa wa Rukwa kufuatilia tuhuma dhidi ya mkandarasi huyo na hujuma uliyofanywa katika mradi wa Maji Laela.Kamanda Nyange akizungumza na wanahabari ofisi kwake amethibitishwa kukamatwa kwa mkandarasi huyo akisema kuwa anatuhumiwa kutekeleza mradi huo pamoja na mingine yenye thamani ya shilingi bilioni tano mkoani Rukwa chini ya kiwango, hivyo kusababisha wananchi kukosa maji waliyotegemea kuyapata.Hata hivyo hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi akiahidi kutoa baadaye huku taarifa zilizopo zinaeleza kuwa watuhumiwa wawili wanaodaiwa kuhujumu mradi wa maji Laela, Jeshi la Polisi liliwachia huru kwa dhamana bado hawajatiwa nguvuni .Jafo apigilia msumari agizo la Magufuli Wakati hatua hizo zikichukuliwa dhidi ya mkandarasi huyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi ) amesisitiza kuwa agizo la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kuhamia katika mji mdogo wa Laela lililotolewa na Rais John Magufuli ni amri ambayo lazima itekelezwe ndani ya mwezi mmoja .Waziri Jafo alisema amelazimika kutoa maelekezo hayo kutokana na kuwepo majadiliano juu ya utekelezaji agizo hilo la Rais Magufuli wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mjini hapa jana ili kuhakikisha linatekelezwa kwa wakati.. Aidha Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Dk Halfany Haule alimweleza bayana Mwenyekiti Ntila na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Nyangi Msemakweli kuwa hatasita kuwaelekeza Suma – JKT kuwahamisha kwa nguvu iwapo uhamaji wao utakuwa wa kusuasua.Waziri Jafo alielekeza Sh milioni 844 ambazo zilikuwa zitumike kukamilisha ujenzi wa ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga inayojengwa mjini Sumbawanga zielekezwe katika ujenzi wa majengo ya ofisi katika mji mdogo wa Laela.“Nimeshaelekeza Serikali Mkoa wa Rukwa ifuatilie mkataba wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo ambao hata mimi haujaniridhisha kwa kuwashirikisha mjenzi wa mradi , mhandisi mshauri wa mradi na wana sheria. Pia nimezuia kiasi cha Sh milioni 155 ambazo zilikuwa zitumike katika ujenzi wa uzio sisitumike na haitajengwa tena bali nimeelekeza zielekezwe katika ujenzi wa Ofisi ya DED katika mji mdogo wa Laela “ alisisitiza .Alielekeza kuwa majengo ya ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yajengwe kwa mfumo wa “Force Account “ na si vinginevyo huku akisisitiza kuwa maelekezo ya Rais Magufuli lazima yatekelezwe kwa haraka iwezekavyo ndani ya mwezi mmoja kama alivyoagiza .Juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Laela kabla hajazindua barabara kuu ya Sumbawanga – Laela – Tunduma aliagiza Halamashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na kuipatia mwezi mmoja iwe imehamia katika mji mdogo wa Laela kwa sasa iko mjini Sumbawanga umbali wa kilomita 100 kutoka sumbawanga mjini Barabara hiyo yenye umbali wa kilometa 223.2 kwa thamani ya zaidi ya Sh bilioni 375 kwa ufadhili wa Seikali ya Marekani kupitia Shirika lake la Changamoto za Milenia (MCC) ulioanza 2010 na kukamilia 2015.Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga , Nyangi Msemakweli alimwahidi Rais Magufuli kuwa ofisi yake itahamia katika mji mdogo wa Laela ndani ya wiki mbili. Pia Jafo amemwagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Mijini na Vjijini nchini (TARURA), Vicent Seif kumsimamisha Mtaribu Mkuu wa Tarura mkoa wa Rukwa, Bonifasi William kwa kipindi cha wiki mbili kupisha uchunguzi dhidi yake.Alisema kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo baada ya kupokea malalamiko mengi ofisi ya Tarura mkoa wa Rukwa ikituhumiwa kandarasi za ujenzi wa barabara zinatolewa kwa upendeleo kwa wakandarasi wasio na sifa wala uwezo wa kitaalamu vitendo vinavyoashiria kuwepo kwa rushwa .Aidha amewagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –Tamisemi kitengo cha ufuatliaji , Josephat Nyamhanga kuunda tume ya wataalamu haraka iwezekanavyo itakayofanyia uchunguzi wa kina malalamiko hayo ambayo inawezekana kandarasi hizo zimetolewa bila kufuata utaratibu wa manunuzi na kusababisha gharama kubwa . Waziri Jafo alitoa maelekezo hayo jana wakati akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yaliyofanyika mjini hapa .
3
Tanasha alijawa hasira baada ya madai ya Lokole kuwa hana ujuzi kitandani Alipuzilia madai hayo na kumshauri rakiye Mondi kumjaribu ili kuthibitisha ukweli Tanasha Donna ameamua kutoa mishale yake na kuimarisha kinga huku marafiki wa karibu wa Diamond wakujitokeza kuanza kumpaka tope. Donna alikasirika si haba baada ya Juma Lokole kueleza kwa hana ujuzi wa mashumbulizi na ndiyo maana Mondi alimtema. Kupitia kwa ukurasa wake wa Instragram, msanii huyu aliyesifika kwa kibao chake cha cha Gere alimrarua Juma Lokole na kufutilia mbali madai yake kabla kuling’oa chapisho lake hilo. Alishangaa ni kwanini Juma hakuwa amejitokeza wazi na kudhibitisha kama kweli hana umahiri kitandani. Kutia chumvi kwenye kidonda, Donna alieleza kuwa Juma ni mume wa masekunde tu na kuwa hakai kama mtu anayeweza kushambulia mpira kwa muda. #tanasha response to claims she is lazy in bed was quite swift A post shared by Urban News (@urbannews254) on May 2, 2020 at 7:14am PDT Hakukomea hapo, Donna alidai kuwa Juma hana shughuli na wanawake na hivyo hawezi akajua kuhusu mashambulizi kama hayo na hivyo kumshauri kuendeleza ‘ligi’ yake. “Oh wait, I forgot you do not do women so I guess you will never know. But hey, you know what they say: empty vessels make a lot of noise,” It’s sad how some people only have negative things to say when they know absolutely NOTHING about you. Remember gossip is shared by the misinformed who often sound like fools, while creating ongoing drama & disorder. ~ Translate that GIIIIRL 😉🥰😘 A post shared by Tanasha Donna Oketch (@tanashadonna) on May 2, 2020 at 8:04am PDT ”Oh subiri, nilisahau kuwa wewe si wa wanadada hivyo hutajua. Lakini je, unajua wanachosema: Debe shinda haiachi kelele,’’ alisema Donna.” Donna aliandika. Juma alieleza kuwa Diamond alikuwa tayari kumuoa Donna lakini kiuno chake kisichopinda kikamkosesha nafasi hiyo. Issa 90s mood all the way… 🎈🔌🎥 A post shared by Tanasha Donna Oketch (@tanashadonna) on Apr 21, 2020 at 1:42pm PDT
1
RAIS John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na wanasiasa wakongwe John Cheyo, James Mbatia, John Shibuda na mfanyabiashara maarufu, Rostam Aziz.Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais Magufuli amekutana na kufanya nao mazungumzo jana Dar es Salaam. Baada ya mazungumzo hayo, Rostam alimpongeza Rais Magufuli kwa uongozi bora, akisema anatengeneza misingi imara ya uchumi unaokua kwa uhakika zaidi kwa kujenga miundombinu ikiwemo barabara, reli na bandari ambayo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi na kuzalisha ajira.Rostam aliyewahi kuwa Katibu wa NEC wa Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora, alisema anaunga mkono juhudi za Rais Magufuli na kubainisha kuwa jukumu la wafanyabiashara ni kutumia fursa nyingi zilizopo katika viwanda, ujenzi na nyinginezo.“Tunamuunga mkono Rais kwa kuhakikisha Watanzania tunawekeza katika nchi yetu, kukuza uchumi wetu, hilo ndilo la msingi kwa sisi wafanyabiashara,” alisema mfanyabiashara huyo tajiri.Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Mbatia alisema katika kutekeleza malengo 17 ya dunia, Tanzania inafanya vizuri katika lengo la elimu ambalo linazungumzia elimu bora na shirikishi.Alisisitiza kuwa Watanzania wote wana kila sababu ya kuendelea kuijenga nchi yao kwa mawazo ya pamoja yanayozingatia ujumbe uliomo katika wimbo wa Taifa unaosisitiza hekima, umoja na amani.Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Shibuda alisema amekutana na Rais Magufuli ili kumpongeza kwa uamuzi mzuri alioufanya kutatua tatizo la soko la korosho. Alimhakikishia kuwa vyama vya siasa vinamuunga mkono kwa uongozi mzuri unaolenga kurekebisha dosari za mmomonyoko wa maadili ndani ya serikali na taasisi mbalimbali, vikiwamo vyama vya siasa.“Katika miaka mitatu, Rais Magufuli amerejesha sifa ya utaifa wetu ya kuwa nchi ya kuaminika na kusadikika na amekweza ari ya uhuru na kujitegemea, tulikuwa na hali duni na dumavu ya maendeleo na ustawi wa jamii, tulikuwa na hali ambayo maendeleo yetu hayawiani na maliasili tulizonazo na rasilimali tulizonazo,” alisisitiza.Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha UDP, Cheyo alimpongeza Rais Magufuli kwa msimamo na ujasiri aliouonesha katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake na ametaka Watanzania wajivunie kuwa na Rais ambaye ameonesha dhamira njema ya kufikia nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.“Sisi Watanzania ni lazima tujivunie Rais tuliye naye, ni Rais anayetoa uamuzi, hata kama utakuwa mgumu kiasi gani, akiamua kusema tunakwenda kujenga Stieglers’ Gorge tutakwenda, akiamua kuwa tunakwenda kujenga standard gauge tunakwenda, akiamua watoto watasoma bure kuanzia darasa la kwanza hadi sekondari inafanyika, na katika miaka mitatu hii imedhihirika kuwa maamuzi yake yanalisaidia Taifa sana,” alisema Cheyo.Wakati huohuo, Rais Magufuli amempongeza Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa kwa mchango wake mkubwa alioutoa wakati wa uongozi wake. Rais Magufuli ametoa pongezi hizo katika Misa Takatifu ya Shukrani ya Uhai kwa Rais mstaafu Mkapa ambaye juzi alitimiza miaka 80 tangu kuzaliwa iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria Imakulata, Dar es Salaam na kuongozwa Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.Rais Magufuli alisema wakati akiwa madarakani Rais mstaafu Mkapa alifanya mambo mengi na muhimu kwa taifa na ataendelea kukumbukwa kwa kazi nzuri. “Leo unapotimiza miaka 80 nakushukuru na kukupongeza sana, nakuombea Mwenyezi Mungu aendelee kukupa afya njema wewe na familia yako, na sisi viongozi tuliopo sasa tutaendelea kuyaenzi mazuri yote uliyoyafanya,” alisema Rais Magufuli.Kwa upande wake Rais mstaafu Mkapa alimshukuru Rais Magufuli na kumtakia heri sambamba na kuwashukuru Maaskofu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mwandamizi, Jude Thadaeus Ruwai’chi na Askofu Msaidizi, Eusebius Nzigilwa walioongoza misa hiyo pamoja na viongozi wengine na waumini wenzake.Rais mstaafu Mkapa amebainisha kuwa anampongeza Rais Magufuli kwa uongozi wake kwa kuwa Tanzania imeendelea kuwa na sifa nzuri ya amani na umoja na kwamba hata akiwa nje ya nchi anapoulizwa siri ya Tanzania kuwa na Marais wastaafu watatu ambao wanaishi vizuri nchini mwao, huwajibu kuwa siri kubwa ni uwepo wa amani, umoja na mshikamano.
3
  KINSHASA, DRC PAMOJA na fomu ya kuwania urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuuzwa bei ya juu ya Dola za Marekani 100,000 sawa na Sh milioni 224, wagombea 26 wamejitokeza kuwania wadhifa huo. Hilo limefahamika siku moja baada ya Rais Joseph Kabila kutangaza kuachia ngazi, huku Tume Huru ya Uchaguzi DRC (CENI) ikitangaza orodha hiyo ndefu ya wagombea nchini humo. Miongoni mwa wagombea hao ni wanawake watatu na mawaziri wakuu wa zamani watatu, wagombea huru wakiwa 16 na wa vyama vya upinzani wanane. Daftari la kudumu la wagombea litatangazwa Septemba 19 tayari kwa maandalizi ya uchaguzi utakaofanyika Desemba 23 mwaka huu. Uchaguzi huo wa duru moja pekee umeorodhesha wagombea mara mbili zaidi kuliko ule wa mwaka 2011. Juzi Jumatano pekee, ambayo ilikuwa siku ya mwisho kwa wagombea kuwasilisha majina yao, walijitokeza 18 pekee akiwamo mgombea aliyeteuliwa na Rais Kabila, Emmanuel Shadari. Waziri huyo wa mambo ya ndani wa zamani amesema akichaguliwa atahakikisha wananchi wanaishi kwa amani na hali yao ya maisha kuboreka. Naibu Katibu Mtendaji wa Chama tawala cha PPRD, Ferdinand Kambere, amesema uteuzi wa Shadary ni alama ya ushujaa wa demokrasia nchini. Kwa upande wake upinzani umelezea kwamba uteuzi wa mgombea wa chama tawala, ni hatua ya ushindi wa demokrasia, lakini wametarajia mageuzi wakati wa uchaguzi. Martin Fayulu ambaye ni mgombea wa vuguvugu Dynamique de l’opposition amesema raia ndie anayetakiwa kuamua kupitia uchaguzi huru. Amesema hawana maoni yeyote kufuatia uteuzi huo wa mrithi wa Kabila, na kwamba ni mambo yao ya ndani, kwa kuwa Kabila anajua umuhimu wa maamuzi yake. Amesema ikiwa amepanga njama ya kurejea madarakani baadae kama alivyofanya Rais wa Urusi Vladimir Putin na Waziri Mkuu Dmitry Medvedev hilo ni haki yake, lakini akionya kwamba wanachotaka uwepo wa uchaguzi huru, wa wazi na wa kidemokrasia ilikuruhusu raia wa Kongo kujichagulia viongozi wao wenyewe. Miongoni mwa wagombea wa upinzani ni pamoja na Jeanpierre Bemba, Vital Kamerhe na Felix Tshisekedi kiongozi wa chama cha UDPS. Wagombea watatu ni wanawake ambao wawili wameishi ugenini akiwemo Bi. Monique Mukuna.
2
Mchezaji huyo pia jana alionekana kwenye mazoezi ya Simba yanayofanyika kwenye uwanja wa Sigara ingawa alikuwa akijificha ndani ya gari bila kujitokeza kwa mashabiki waliozingira gari hilo.Kiiza, ambaye aliachwa msimu uliopita na Yanga na nafasi yake kuchukuliwa na mchezaji wa Liberia Kpah Sherman, amesajiliwa kama mchezaji huru kwani hakuwa na timu yoyote baada ya kutemwa na vijana hao wa Jangwani.Akijibu maswali ya waandishi wa habari jana msemaji wa Simba, Haji Manara alisema Kiiza kwa sasa ni mchezaji wao kwa vile wamekwishampa mkataba wa miaka miwili.“Kiiza amefuzu vipimo leo mchana (jana) kwa hiyo tumempa mkataba wa miaka miwili, ni mchezaji wetu halali, tunategemea atakiongoza kikosi cha Simba kufanya vizuri msimu ujao,” alisema.Aidha, katika uwanja wa Sigara Kiiza alijitokeza huku mashabiki wa Simba wakionesha shauku ya kutaka kumsalimia lakini alijificha katika gari bila kushuka na baadaye alisalimia huku akiwa ndani ya gari bila kushuka.Kwa mujibu wa mtandao wa Simba, Kiiza alisema amekuja na kitu tofauti kwa ajili ya wapenzi na wanachama wa klabu hiyo na hivyo wakae mkao wa kula kwa vile anaijua vizuri ligi ya Tanzania.“Nitashirikiana na wachezaji wenzangu kufikia malengo ya kutwaa ubingwa msimu ujao,”alisema.Wakati huo huo, Simba inatarajia kuweka kambi Lushoto mkoani Tanga kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Simba, Collin Frisch alisema kambi hiyo wataitangaza wakati wowote na kwamba lengo ni kuhakikisha timu inajipanga na kufanya vizuri msimu ujao.
4
MVUA iliyonyesha kwa vipindi tofauti juzi na jana katika maeneo mbali mbali ya Jiji la Dar es Salaam, imekatisha kwa muda mawasiliano katika baadhi ya maeneo ikiwamo Barabara ya Morogoro hususani eneo la Jangwani.Hali hiyo imesababisha magari yanayotumia barabara hiyo, kutumia barabara mbadala ili kuendelea na safari. Mvua hiyo iliyonyesha kuanzia juzi jioni hadi jana mchana, kwa kiasi kikubwa ilisababisha eneo hilo la Jangwani, kufurika maji yaliyokuwa yakipita juu ya daraja sambamba na maeneo mengine ya barabara hiyo na hivyo kusababisha magari yakiwemo mabasi ya mwendokasi kushindwa kupita.Aidha, katika hatua nyingine Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema uwepo wa mvua hizo zinazonyesha mfululizo katika baadhi ya maeneo ya Pwani ya Kaskazini ikihusisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, zimesababishwa na kuimarika kwa ukanda wa mvua (ITCZ). Kwa mujibu wa Meneja wa Kituo Kikuu cha Utabiri kutoka TMA, Samweli Mbuya, mvua hizo zinatarajiwa kuendelea hadi kesho na baadaye mvua kama hizo kujirudia tena katikati ya mwezi huu.“Athari za mvua zilizonyesha katika kipindi cha wiki moja mfulululizo katika ukanda wa pwani ya Kaskazini pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba zimesababisha kutuama kwa maji na mafuriko, hivyo kutokana na ardhi kuwa na unyevunyevu mwingi, ongezeko kidogo la mvua linaweza kuendelea kusababisha athari kama zilizokwishajitokeza,” alisema Mbuya.Aliwataka wananchi hao, kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa na kuzingatia tahadhari zilizotolewa na mirejeo yake pamoja na kupata ushauri wa miongozo ya wataalamu katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo. Awali gazeti hili lilitembelea maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam likiwemo Jangwani na kushuhudia maji hayo yakiwa yamefurika katika eneo hilo.
3