text
stringlengths
1k
17.3k
label
int64
0
5
SHIRIKA la Posta Tanzania limeomba radhi kwa kuchapisha kimakosa kwenye magazeti ya serikali majina ya taasisi, ambazo si wadaiwa wa kodi ya pango ya shirika hilo pamoja na malimbikizo yake.Mkuu wa Kitengo cha Miliki wa Shirika la Posta Tanzania, ameomba radhi jana kupitia gazeti hili, ukurasa wa 19.Katika maelezo yake, Shirika hilo lilisema linaomba radhi kwa makosa yaliyofanyika kwenye tangazo lake kwenye magazeti ya HabariLeo na Daily News ya Julai 2 mwaka huu yenye kichwa cha habari “TAARIFA KWA WAPANGAJI WA NYUMBA ZA POSTA WANAODAIWA KODI NA MALIMBIKIZO”.Kutokana na tangazo hilo, HabariLeo la Julai 4 liliandika habari iliyotaja baadhi ya taasisi hizo zenye madeni makubwa.Baada ya kutokea kwa mkanganyiko huo, jana Shirika hilo la Posta Tanzania liliomba radhi kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Benki ya TPB, Benki ya CRDB, Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Zantel na taasisi nyingine, kuwa majina ya taasisi hizo yalitolewa kimakosa, kwani si miongoni mwa wanaodaiwa wa Shirika la Posta.Shirika hilo lilisisitiza kuwa linaomba radhi kwa wahusika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
3
       Kocha wa Derby County Frank Lampard anaelekea kuteuliwa kuwa meneja wa Chelsea baada ya Maurizio Sarri kukataa ombi la kubakia kikosini. Lampard anamtaka mchezaji mwenzake wa zamani katika klabu hiyo, Didier Drogba awe mmoja wa wasaidizi wake , lakini si John Terry. (Sun) Mchezaji wa Manchester United na timu ya taifa yaUfaransa Paul Pogba, 26, anasisitiza kuwa anataka kuondoka United na kuelekea Real Madrid. (Marca) Crystal Palace imemthamanisha kwa kiwango cha pauni milioni 50 mchezaji wa safu ya Ulinzi ya kikosi cha England cha vijana chini ya miaka 21 – Aaron Wan-Bissaka, ambaye angependa kuhamia Manchester United, lakini hajaonyesha msukumo wa kuondoka katika kikosi cha Palace. (Sky Sports) Aaron Wan-Bissaka, ambaye angependa kuhamia Manchester United, hajaonyesha msukumo wa kuondoka katika kikosi cha Eagles. Aaron Wan-Bissaka, ambaye angependa kuhamia Manchester United, hajaonyesha msukumo wa kuondoka katika kikosi cha Eagles.Tottenham wameachana na mpango wa kutaka kumsajili kiungo wa klabu ya Lisbon, Bruno Fernandes, mwenye miaka 24, ambaye pia amekuwa akihusishwa na uhamisho kuelekea Manchester United. (Mail) Manchester United wanaamini wanaweza kushinda kinyang’anyiro cha kumsainisha mkataba mlinzi Harry Maguire kwasababu ya kusitasita kwa Manchester City kulipa pauni milioni 80 za ziada kwa ajili ya kumchukua mchezaji huyo wa kimataifa wa England mwenye umri wa miaka 26 (Mail). Kiungo wa kati wa Chelsea Mbrazil Willian, mwenye umri wa miaka 30, anakaribia kusaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kusalia katika uga wa Stamford Bridge (Sun). Manchester United wako tayari kumuongezea pesa kipa David de Gea, mwenye umri wa miaka 28, kwa azma ya kumshawishi aendelee kubakia katika uga wa Old Trafford baada ya Juni 2020 (ESPN). Manchester United watamtaka De Gea abaki kikosini hata kama ni kutoa pesa za ziada. Manchester United watamtaka De Gea abaki kikosini hata kama ni kutoa pesa za ziada. Ajax watataka kitita cha pauni milioni 30 tu kwa ajili ya kumuachia winga wao raia wa Morocco Hakim Ziyech. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akihusishwa na tetesi za kutakiwa na vilabu vya Liverpool na Arsenal (Mirror). Manchester United wanataka sana kusaini mkataba na mchezaji wa kimataifa wa Argentina Giovani Lo Celso, mwenye umri wa miaka 23, lakini Real Betis wameweka dau la pauni milioni 67 kwa kiungo wao wa huyo ambaye pia amekuwa akihusishwa na klabu ya Tottenham (inews). Liverpool wamekwishaonesha nia ya kumtaka winga wa Ivory Coast Nicolas Pepe, 24 ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya Lille. (Le10 Sport, via Daily Express) Arsenal hawatakubali Pierre-Emerick Aubameyang achukuliwe na timu nyingine. Mshambuliaji wa Fulham Mserbia Aleksandar Mitrovic, ambaye amekuwa akihusishwa na West Ham, anakaribia kuhamia Real Betis. (Star) Arsenal wanapanga kuzungumza na mshambuliaji kutoka Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, mwenye umri wa miaka 29, ili kumpatia mkataba mkubwa kwa lengo la kuipiku klabu kadhaa za Ligi ya Uchina zinazotaka kumchukua (Mirror). Leeds watakataa ofa yoyote kutoka Tottenham ya kumchukua Jack Clarke, 18, anayecheza safu ya ushambuliaji na pia kutoka Aston Villa ofa ya kumchukua kiungo Kalvin Phillips mwenye umri wa miaka 23 (Star). Manchester United wanataka sana kusaini mkataba na Mchezaji wa kimataifa wa Argentina Giovani Lo CelsoHaki. Kaka yake na wakala wa mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Gonzalo Higuain ameonekana kumaliza uvumi wa kumuhusisha mchezaji huyo wa kuhamia klabu ya AS Roma kwa usema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 anataka kumalizia maisha yake ya soka na Juventus (Mirror). Kiungo wa kati wa Chelsea Mbrazil Willian, mwenye umri wa miaka 30, anakaribia kabisa kusaini mikataba miwili ya kubakia katika Stamford Bridge. Meneja mpya wa Roma Paulo Fonseca anaangalia uwezekano wa dau kwa ajili ya kumnasa kiungo wa kati wa Manchester United na raia wa Brazil, Fred, mwenye umri wa miaka 26. (Metro) Mlinzi wa England Kyle Walker yuko tayari kusaini mkataba wa miaka miwili zaidi katika klabu ya Manchester City (Manchester Evening News). Mlinzi wa England Kyle Walker yuko tayari kusaini mkataba wa miaka na klabu ya Manchester City. Manchester United wanaimani kuwa Sean Longstaff anataka kuhamia Old Trafford – licha ya kwamba kiungo huyo kueleza wazi kuwa moyo wake ungali na klabu ya Newcastle. Brighton wako katika mazungumzo na Genk juu ya mkataba na nahodha wa kikosi cha Ubelgiji na winga Leandro Trossard, mwenye umri wa miaka 24. (Sky Sports) Kiungo wa kati wa River Plate Santiago Sosa, mwenye umri wa miaka 20, amehusishwa na uhamisho wa pauni milioni 13 kuelekea Everton, na inasemekana anaweza kupata pasipoti ya EU kutokana na asili yake ya Ulaya , ambayo inaweza kumuongezea bahati yake ya kuhamia katika Primia Ligi msimu ujao (Liverpool Echo). Rafiki wa kike wa Mlinzi wa Ajax Matthijs de Ligt na mama yake wameonekana Paris wakitafuta nyumba . Mchezaji hyo wa miaka 19 amekuwa akihusishwa na timu ya Ufaransa ya Paris St-Germain (De Telegraaf, via AS).
4
MSHINDI watatu wa dunia wa mbio za meta 10,000 Rhonex Kipruto na bingwa wa Afrika wa mwaka 2016 wa meta 5,000, Sheila Chepkirui wamevunja rekodi za wanaume na wanawake za barabarani za kilometa 10 katika mashindano yaliyofanyika hapa. Kipruto mwenye umri wa miaka 20 alishinda mbio za Valencia Ibercaja za kilometa 10 za barabarani juzi Jumapili katika muda mpya wa dunia wa dakika 26 na sekunde 23. Chepkirui, mshindi namba mbili wa mbio za nyika wa mwaka 2016, alimaliza kwa kutumia dakika 29:42 katika mbio za wanawake katika mbio hizo zilizofanyika katika jiji hilo la Hispania. Kipruto, ambaye pia ni mshindi wa dunia wa meta 10,000 kwa wanariadha wenye umri chini ya miaka 20, aliweka muda mpya ikiwa ni wiki sita baada bingwa Mganda Joshua kushinda mbio za meta 10,000 wakati wa mashindano ya Nusu Marathoni ya Valencia Desemba mosi mwaka jana. Kipruto alimaliza umbali wa kilometa tano kwa kutumia dakika 13:18 wakati akielekea kuvunja rekodi ya Cheptegei kwa sekunde 15. Cheptegei, bingwa wa mbio za nyika wa dunia, alivunja rekodi ya kilometa 10 za dunia huko Valencia, akiweka muda mpya wa dakika 26:38. Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 23 Mganda alivunja rekodi ya awali kwa sekunde sita, ambayo iliwekwa na Mkenya Leonard Komon aliposhinda mbio za kilometa 10 za Utrecht Singelloop kwa muda wa 26:44 Septemba 26, 2010 huko Uholanzi. Matokeo: 1. Rhonex Kipruto (Kenya) 26:24 (Rekodi ya Dunia) 2. Bernard Kimeli (Kenya) 27:123. Julián Wanders 27:13 (Ulaya) Wanawake: 1. Sheila Chepkirui (Kenya) 29:42 2. Rosemary Wanjiru (Kenya) 29:46 3. Norah Jeruto (Kenya) 29:46
4
Hayo yalisemwa na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Mazrui wakati alipozungumza na wajasiriamali walioshiriki katika Maonesho ya Siku ya Wafanyakazi duniani Mei Mosi yaliyofanyika katika viwanja vya Amaan.Alisema miongoni mwa njia zitakazowawezesha wajasiriamali kuonesha bidhaa zao na kuziuza ni kufanya maonesho ya kibiashara yatakayohudhuriwa na wananchi mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara.“Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko imefungua milango kwa wajasiriamali na taasisi mbalimbali kuandaa Maonesho ya kibiashara yatakayotangaza biashara zao na kupata soko,” alisema.Kwa mfano alisema Maonesho ya Mei Mosi yalionesha kwamba taasisi na wajasiriamali mbalimbali na taasisi wanao uwezo wa kutangaza bidhaa zao wanazotengeneza au kuzalisha.“Nimefurahishwa na bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali mbalimbali ambazo zimetengenezwa na wafanyabiashara,” alisema.Baadhi ya bidhaa zilizooneshwa na wajasiriamali na kuonesha ubunifu mkubwa ni utengenezaji wa zao la mwani kwa matumizi mbalimbali ikiwemo keki na mkate.Mmoja ya wajasiriamali wanaozalisha na kutengeneza zao la mwani kwa matumizi mbalimbali ikiwemo keki, Bimkubwa Haji alisema zao la mwani limeongezeka thamani yake kufuatia kuongezeka kwa matumizi mbalimbali.
5
Ushauri huo ulitolewa hivi karibuni na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, William Lukuvi wakati wa hafla ya kumpongeza Samatta baada ya kupata tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani.Waziri Lukuvi ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu katika hafla hiyo, alitoa ushauri huo kwa Vodacom ambao ni wadhamini wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara (VPL) kama sehemu ya kumuenzi Samatta ambaye ameliletea taifa heshima na kuitangaza nchi baada ya kutunukiwa tuzo hiyo ya heshima barani Afrika.Waziri alitoa rai kwa wadau wa soka nchini wakiwemo Vodacom kumuenzi Samatta kwa vitendo kutokana na heshima aliyoiletea Tanzania ikiwemo kujenga uwanja aliokuwa anachezea kabla ya kiwango chake kuwa kikubwa.Mkuu wa Mauzo wa Kanda ya Pwani wa Vodacom Tanzania, Herieth Koka, alisema ushauri huo wa Serikali ni mzuri katika kumuenzi Samatta na Vodacom itaufanyia kazi.“Vodacom ikiwa ni mdhamini mkuu wa ligi ya soka nchini tumefurahishwa na mafanikio ya Samatta kwa kuwa moja ya dhamira ya kampuni yetu ni kusaidia michezo hususan mchezo wa soka, kwani tunaamini kuwa bado kuna fursa ya vijana wengi wa kitanzania kufanya maisha yao kuwa murua kupitia michezo,” alisema.Pia Mkuu huyo wa Mauzo wa Kanda ya Pwani, alisema kampuni hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa soka nchini kuhakikisha Ligi Kuu ya Vodacom inazidi kuwa bora ili wapatikane wachezaji wengine wa kuitangaza Tanzania katika ramani ya soka duniani kama alivyofanya Samatta.
4
KESI ya tuhuma za kumteka nyara mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji maarufu MO inayomkabili dereva teksi, Mousa Twaleb (46) Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam ilitajwa tena jana na ikaelezwa na upande wa mashitaka kuwa upelelezi haujakamilika.Wakili wa Serikali, Dais Makakala alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika hivyo kuomba tarehe nyingine ya kutajwa.Baada ya maelezo hayo, Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 25, mwaka huu na mshitakiwa ambaye ni mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam, amerudishwa rumande. Twaleb anakabiliwa na mashitaka matatu ikiwemo kumteka nyara mfanyabiashara maarufu nchini, MO.Katika mashitaka ya kwanza, inadaiwa mshitakiwa huyo alijihusisha na genge la uhalifu. Inadaiwa Mei Mosi, 2018 na Oktoba 10, 2018, maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na Johannesburg nchini Afrika Kusini, kwa makusudi alitoa msaada wa kutendeka vitendo vya jinai au uhalifu wa kupangwa ili kujipatia faida.Pia inadaiwa Oktoba 11, mwaka jana maeneo Hoteli ya Colloseum wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, akiwa na watu wengine ambao hawapo mahakamani, walimteka nyara MO kwa nia ya kumhifadhi kwa siri na kumweka maeneo ambayo ni hatari.Pia inadaiwa Julai 10, mwaka jana Mbezi Beach wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, Twaleb alitakatisha fedha, Sh 8,000,000 wakati akijua fedha hizo ni kosa la kushiriki genge la uhalifu na makosa ya kupanga.MO alitekwa nyara Oktoba 11, mwaka jana alfajiri maeneo ya Hoteli ya Colloseum wakati akienda kufanya mazoezi na alipatikana Oktoba 20, mwaka huo huo katika eneo la Gymkhana.Wakati huo huo, Mkurugenzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam (UDART), Robert Kisena (46) na wenzake wanne wanaokabiliwa na mashitaka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ya kuisababishia serikali hasara wanaendelea kusota rumande kwa sababu upelelezi wake haujakamilika.Wakili wa Serikali, Ester Martin alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizire kesi hiyo ilikuja kutajwa na upelelezi haujakamilika hivyo kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.Hakimu Rwizire aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 24, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na washitakiwa wamerudishwa rumande kwa sababu mashitaka hayo hayana dhamana kisheria.
3
LONDON, ENGLAND BAADA ya klabu ya Arsenal kutolewa katika michuano ya Kombe la FA juzi dhidi ya Watford, mashabiki wa klabu hiyo ya jijini London wamemjia juu kocha, Arsene Wenger na kumtaka aondoke. Arsenal walikuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo, lakini wameshindwa kulitetea na kukubali kichapo hicho cha mabao 2-1 na kuwafanya mashabiki kumtaka Wenger afungashe virago vyake. Mashabiki hao wamemshambulia kocha huyo kupitia mitandao ya kijamii, lakini amewataka kuwa wavumilivu na kuiunga mkono timu yao hasa katika michezo ijayo. “Arsenal imepoteza michezo mingi na imetolewa kwenye michuano ya Kombe la FA, mashabiki wanatakiwa kuvumilia na kuangalia michezo ijayo ya Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa. “Hii ni timu yao wanatakiwa kukubaliana na chochote kinachotokea sio siku zote tutakuwa na furaha, kuna wakati mambo yanakuwa magumu lakini tunatakiwa kuwa pamoja katika kila mchezo, najua inauma sana hasa unapopoteza mchezo ukiwa nyumbani ila ndivyo soka lilivyo,” alisema Wenger. Wenger anaamini nguvu zake anazielekeza katika michuano ya Ligi Kuu nchini England na Ligi ya Mabingwa, ambapo kesho klabu hiyo itashuka dimbani kupambana na mabingwa Barcelona kwenye Uwanja wa Nou Camp, huku mchezo wa awali Arsenal wakiwa nyumbani walikubali kichapo cha mabao 2-0.
4
Na Kadama Malunde -Shinyanga MATUKIO ya watu kujiua yameendelea kushika kasi katika Mkoa wa Sninyanga ambako kijana mwingine, Paul Ezekiel (17) mkazi wa Mtaa wa Mazinge Kata ya Ndembezi mjini hapa, amefariki dunia kwa kujinyonga kwa kamba juu ya mti jirani na nyumba yake kwa kile kinachodaiwa ni ugumu wa maisha. Tukio hilo lilitokea jana saa 10 alfajiri ambako inaelezwa kuwa Ezekiel alitoka nje ya lango la nyumba yao na kuelekea kwenye mti ambako alijipiga kitanzi kilichosababisha kifo chake. Baba mzazi wa Ezekiel Paul, alisema awali kijana wake alikuwa na ugomvi na marafiki zake waendesha baiskeli maarufu ‘daladala’, ambao baadaye walisuluhishwa na akaendelea na majukumu yake. Alisema chanzo cha kifo cha kijana wake hajakifahamu vizuri ingawa alisema kijana wake huyo pamoja na kujishughulisha na kazi mbalimbali za kujipatia kipato, alikuwa akilalamika mara kwa mara kuwa maisha ni magumu. “Ilipofika saa 10 usiku nilisikia mlango wa chumba cha kijana wangu ukifunguliwa, nikajua ametoka kwenda kujisaidia, lakini ukapita muda mrefu sikusikia kuwa amerudi ndipo nikatoka nje na kukuta lango la uwani likiwa wazi, nikaanza kumtafuta bila mafanikio. “Niliporudi ndani nikamwamsha mama yake mzazi na wadogo zake wawili wa kike, tukaanza kumsaka ndipo tukamuona akiwa juu ya mti jirani na nyumba yetu akiwa amekwisha kufariki dunia kwa kujinyonga na kamba,” alisema Paul. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Jumanne Murilo, alisema hadi sasa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa kutokana na tukio hilo. Matukio ya watu kuchukua uamuzi wa kujiua yameanza kukithiri katika manispaa ya Shinyanga na ndani ya mwezi mmoja hilo ni tukio la nne. Hadi sasa waliofariki dunia kwa utaratibu huo ni Luhende Lusangija (34), Mwenyekiti wa waendesha bodaboda Manispaa ya Shinyanga, Jacob Paul na Saada Elias ambaye alijijichinja kwa kisu na chupa ya soda.
3
['Man United wako tayari kutoa kiasi cha Pauni million 45 ili kumnasa nyota wa Leicester City James Maddson na watamtoa Jesse Lingard ili kuweza kufanikisha usajili huo.', '(Sunday Mirror)', 'West ham watapigana vikumbo na Man City katika kuwania saini ya beki kisiki wa Napoli Kalidou Koulibali. (Sunday Express)', 'Inter Milan wanataka kumsajili kiungo wa Spurs Christian Eriksen kwa dau la pauni million 20 katika dirisha hili la januari licha ya nyota huyo atakuwa huru kuondoka bure mwishoni mwa msimu. (Sun on Sunday)', "Wagonga nyundo wa London, West ham wanatarajia kukutana na viongozi Wa Benfica wikiijayo ili kukamilisha dili ya usajili wa mkopo wa kiungo Gedson Fernande's mwenye miaka 20. (Record, via Daily Star Sunday)", 'Bosi wa Everton, Carlo Ancelotti anataka kumsajili kwa mkopo James Rodriguez kutoka Real Madrid. (Sun on Sunday)', 'Tottenham wanamatumaini ya kumsajili moja kwa moja kiungo Giovan lo Celso kutoka Real Betis ambaye anakipiga na Spurs kwa mkopo.(Sun on Sunday)', 'Crystal palace wanamuwania kimsajili kwa mkopo mshambuliaji Cenk Tosun kutoka Everton.(Sunday Mirror)', 'Beki wa Arsenal Mjerumani Shkodran Mustafa mwenye miaka 27 anaweza kuachana na washika mitutu wa London mwishoni mwa mwezi huu.(Sunday Mirror)', 'Bosi wa Leicester City Brendan Rodgers hajathibitisha taarifa za kukubali au kukataa kuwa timu yake itamsajili beki wa Juventus Merih Demirah. (Mail on Sunday)Tottenham wanamatumaini mshambuliaji wale kinda wa Miaka 17 Troy Parrot atasalia kwenye klabuni hapo kwa kwa kusaini mkataba mpya wa muda mrefu mwezi ujao.(Lancashire Telegraph)', 'Meneja wa Newcastle United Steve Bruce amesema kipaumbele cha timu hiyo ni kusajili mshambuliaji mwezi huu wa januari.(Sky Sports)', 'Meneja wa Wolves Nuno Santo ametupilia mbali mpango wa kumuuza beki wa kiitaliano Patrick Cutrone mwenye Miaka 22.(Football Insider)', 'Juventus wamefanya mazungumzo ya awali na Chelsea ili kuangalia uwezokano wa kumsajili beki wa kushoto wa timu hiyo mbrazil Emerson.']
4
['Arsenal inataka kumsaini winga wa Barcelona Malcom, 22, huku Everton ikiwa tayari imewasilisha ofa ya dau la £31.5m kumsaini raia huyo wa Brazil. (Sun)', 'Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Dean Saunders anaamini kwamba Ole Gunnar Solskjaer hatomaliza msimu huu kama mkufunzi wa Manchester United . (talkSPORT) ', 'Solskjaer ana matumaini atafanikiwa kumnunua beki wa leicester Harry Magwire mbele ya majirani za wao wakuu Manchester City. (Mail)', 'Kiungo wa kati wa Manchester United na Uhispania Juan Mata, 31, amekataa mshahara wa £550,000 kwa wiki kutoka kwa klabu ya Shanghai SIPG na akaamua kuandikisha kandarasi mpya na klabu hiyo ya Old Trafford. (90Min)', 'Mata anasema kuwa alitia saini kadarasi mpya kwa kuwa klabu hiyo ni miongoni ma klabu kubwa nne duniani. (MUTV)', 'Ofa ya Everton ya dau la Yuro 30m limekataliwa na Juventus kumnunua mshambuliaji wa Itali Moise Kean. (Tuttosport, via Sport Witness)', 'Newcastle United ilimpatia mkufunzi Sam Allardyce ofa ya kurudi na kuifunza klabu hiyo wiki iliopita , lakini alikataa fursa hiyo.. (Mail)', 'Roma Ina hamu ya kumsajili beki wa Tottenham Toby Alderweireld na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 ana kifungu cha kumuachilia chenye thamani ya £25m . (Sky Sports)', 'Everton imewasilisha ombi la kumsaini mshambuliaji wa Lille Nicolas Pepe. Mchezaji huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 24 ataigharimu the tofees dau litakalovunja rekodi la £58.5m. (Telegraph)', 'Kiungo wa kati wa Southampton ,25 Mario Lemina, ambaye anatakiwa na Man United Arsenal na Leicester, amesema kuwa hataki kuichezea klabu hiyo msimu ujao.. (France Football, via Daily Echo)', 'Tottenham wanaimarisha ombi lao la kutaka kumsaini kiungo wakati wa Real Madrid Dani Ceballos, 22, kwa mkopo. (Mirror)', 'Arsenal inajiandaa kuongeza mabeki Calum Chambers, 24, Carl Jenkinson, 27, ama kiungo wa kati Mohamed Elneny, 26, katika makubaliano ya kumsaini winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha. Ombi la The Gunners la £40m kumnunua mchezaji huyo 26 limekataliwa . (Mirror)', 'Manchester City iko tayari kumzuia kiungo wa kati Fabian Delph msimu huu licha ya uvumi unaomuhusisha mchezaji huyo mwernye umri wa miaka 29 na uhamisho wa kuondoka Etihad. (Metro)', 'David Luiz anaamini kwamba kurudi kwa Frank Lampard katika klabu ya Chelsea utaifanya klabu hiyo kutambua umahiri wake.. (Standard)']
4
WASHINGTON, MAREKANI             |                 SERIKALI ya Marekani imetangaza kusitisha msaada uliokuwa unatolewa kwa lengo la kuimarisha hali ya maisha ya wananchi wa Palestina, hususan wanaoishi katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi. Taarifa ya Serikali hiyo imetolewa na Ofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje, akisema msaada wa kiasi cha dola milioni 200 kwenda Palestina umefutwa, hatua ambayo imelalamikiwa na Balozi wa Palestina na kuushutumu utawala wa Rais Donald Trump kuwa haupendi amani. Ofisa Mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani amesema uamuzi huo ulioagizwa na Rais Trump, uliamuliwa baada ya kufanywa tathmini ya programu za usaidizi katika maeneo ya Palestina. Ofisa huyo ameongeza kwamba, fedha hizo za misaada sasa zitatumika kufadhili miradi yenye umuhimu mahali pengine. “Tumechukua hatua hii baada ya kufanya tathimini ya misaada ya Marekani kwa Mamlaka ya Palestina, hususan maeneo ya Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza, tumeona ni vema fedha hizo zitumike kwenye miradi mbalimbali yenye manufaa kwa wananchi wa Marekani pamoja na kuheshimu thamani ya kodi yao,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo. Uhusiano kati ya mamlaka ya Palestina na utawala wa Marekani uliharibika baada ya Trump kutangaza kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel. Palestina wanasema mji wa Jerusalem Mashariki ni makao yao kama nchi huru, wakati Israel wamesema mji wa Jerusalem ni makao yao makuu. Uamuzi huo wa kusitisha msaada wa kifedha kwa Palestina unakuja katika wakati ambao kuna mgogoro mkubwa wa kibinadamu huko Gaza, huku kukiwa na vurugu za maandamano ya mpakani ya kila wiki yaliyoanza Machi. Wapalestina wapatao 171 wamepoteza maisha kutokana na mashambulizi ya wanajeshi wa Israel, wakati wa maandamano hayo yanayofanyika katika mpaka wa kati ya Palestina na Israel.
2
MUMBAI, INDIA MWANAMUME mmoja mwenye umri wa miaka 31 nchini India ametolewa uvimbe wa kilo 1.8 na timu ya madaktari nchini humo, baada ya kumfanyia upasuaji mkubwa na wa kipekee wenye lengo la kuondoa uvimbe huo. Tukio hilo limetokea huko Magharibi mwa Mumbai, baada ya madaktari kumfanyia upasuaji  Santlal Pal, aliyekuwa na tatizo hilo kwa muda mrefu. Madaktari wanasema uvimbe huo huenda ukawa uvimbe mkubwa zaidi kuwahi kutolewa kwenye ubongo wa binadamu. Upasuaji huo ulifanyika mnamo Februari 14 na kudumu kwa saa saba, katika hospitali ya Nair mjini Mumbai, magharibi mwa nchi hiyo. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Utangazaji la Uingereza (BBC), awali zoezi la upasuaji huo halikutangazwa moja kwa moja, kwa sababu madaktari hawakuwa na uhakika iwapo litafanikiwa na mgonjwa huyo kuwa hai. “Sasa ni suala la kupona tu, lakini maisha yake hayamo hatarini tena,” alisema Dk. Trimurti Nadkarni, ambaye aliongoza timu ya upasuaji wa mfumo wa neva. Santlal Pal, muuza duka kutoka Jimbo la Uttar Pradesh, kaskazini mwa India, amekuwa akiishi na uvimbe huo kwa miaka mitatu. Madaktari wanasema Santal Pal alipoteza uwezo wake wa kuona kutokana na uvimbe huo. Hata hivyo, kuna matumaini kwamba huenda akapata uwezo wa kuona tena baada ya kupona. Mke wake ameliambia gazeti moja India kwamba aliwahi kuambiwa na madaktari katika hospitali tatu tofauti zilizopo Jimbo la Uttar Pradesh kwamba uvimbe huo hauwezi kuondolewa. “Matatizo kama hayo huwa hatari sana. Santal Pal alihitaji gramu 11 za damu wakati wa upasuaji huo,” alisema daktari huyo. Aidha, alitumia mtambo wa kumsaidia kupumua kwa siku kadha baada ya upasuaji huo.
2
Hayo yamesemwa Dar es Salaam na Meneja wa bia ya Kilimanajro Premium Lager, Pamela Kikuli, na kueleza kuwa kipindi hichi kitaitwa ‘Kili Chats.’Alisema sio mara ya kwanza kwa bia hiyo kuandaa kipindi cha aina hii kwani mwaka jana kilirushwa wakati wa msimu wa ‘Nani Mtani Jembe’, kampeni inayowashirikisha wakongwe wa soka hapa nchini Simba na Yanga.Meneja huyo alisema sasa hivi wameamua kujikita katika muziki kwani ndio msimu wa KTMA kwa hivyo wanataka kusikia kutoka kwa wananchi kuhusu maoni yao.“Huu ni mwanzo mzuri kuelekea KTMA ambapo tutaalika wadau mbalimbali kwa mfano Ma DJ, wanamitindo, washiriki katika video mbalimbali na wengine,” alisema Pamela.Alisema kipindi hicho kitarushwa na televisheni ya ITV kila Jumanne saa moja usiku hadi saa moja na nusu kuanzia Mei 12, mwaka huu.Alisisitiza kuwa, wasanii hawatahusishwa katika kipindi hicho ili kuhakikisha wote wanapewa haki sawa kuelekea usiku wa tuzo.“Wasanii hawatahusishwa kabisa kwa kuwa wao wanashindanishwa kwenye KTMA na wote tutajua matokeo usiku ule wa tuzo kwa hivyo hata kwenye kipindi hatutatoa maelezo yoyote kuhusu kura,” alisema.Hata hivyo, kwa mujibu wa Pamela kipindi hicho kitatumika kutoa maelezo kuhusu namna ya kupiga kura.Alisema hadhira (audience) itakayoshiriki katika kipindi hicho itapatikana kupitia ukurasa wa Kili wa facebook na kisha kupewa nafasi ya kushiriki wakati wa kuandaa show.Fainali za Kili Music Awards 2015 zinatarajiwa kufanyika Dar es Salaam Juni 13 mwaka huu.Bia ya Kilimanjaro Premium Lager imedhamini tuzo hizi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1999 na ndio moja ya tuzo zilizodumu kwa muda na kujizolea umaarufu mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na ya Kati
4
SUALA la tembo wanaotoka Hifadhi ya Selous kuendelea kuvamia mashamba na makazi ya wananchi wa maeneo mbalimbali wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, limeendelea kuwa tishio kubwa kwa maisha ya wananchi na mali zao.Kutokana na hali hiyo, baadhi ya wananchi wakiwemo madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru, waliiomba serikali kuwaondoa tembo hao katika makazi yao kwani wamekuwa wakiharibu kwa kiasi kikubwa mazao shambani na kusababisha vifo vya watu wasio na hatia.Kilio hicho kimetolewa jana na baadhi ya madiwani katika kikao cha robo ya pili ya Baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya Tunduru kilichofanyika ukumbi wa Klasta hapa. Aidha, wamelalamikia kucheleweshwa kwa kifuta machozi kwa watu walioharibiwa mali zao na vifuta machozi kwa waliouawa na tembo huku wakiiomba serikali kupeleka chakula kwa baadhi ya shule zinazozungukwa na hifadhi.Diwani wa Kalulu, Rabii Makumba na Diwani wa Marumba, Said Msenga walieleza tembo hao wamevamia nyumba za watu na kula mazao yaliyohifadhiwa ndani, jambo linaloweza pia kusababisha janga kubwa la njaa katika vijiji.Alisema mbali na kula mazao na uharibifu, wanafunzi pia wanashindwa kwenda shule wakihofia usalama wao kwani makundi ya tembo yanakaa barabarani na kuzuia njia hivyo kusababisha utoro kwa wanafunzi wa kata hizo.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Tunduru, Mkwanda Sudi alisema kuna maeneo mengi yamevamiwa na tembo katika wilaya ya Tunduru na sio kata ya Kalulu pekee yake.Alisema kuongezeka kwa makundi ya tembo katika makazi ya watu kunatokana na shughuli za ufugaji kufanyika ndani ya hifadhi na ndiyo sababu ya tembo kufika makazi ya binadamu. Kaimu Ofisa Ardhi na Maliasili wa wilaya ya Tunduru, Fatma Olonya alikiri zaidi ya watu 1,000 wameathirika na serikali itaendelea kukabiliana na makundi ya tembo hao.Alisema, Mamlaka ya Uhifadhi Wanyama Pori (TAWA) inaendelea kuhakikisha tembo hao wanapungua kama mpango wa kudhibiti wanyama ambao ni kero kubwa kwa wananchi.
3
ALIYEWAHI kuwa mkuu wa wilaya tofauti nchini wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza na baadaye kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, Waziri Juma Waziri amefariki dunia. Waziri alifariki dunia wakati akitibiwa katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam, Ijumaa na amezikwa jana nyumbani kwake Sungwi wilayani Kisarawe Mkoa wa Pwani.Kwa mujibu wa watu wa karibu, Mzee Waziri ambaye mwaka huu alitimiza miaka 89, alifariki dunia siku chache tu baada ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa. Akiwa amehudumu katika nafasi mbalimbali serikalini zikiwamo za ubalozi na ukuu wa wilaya zikiwamo Ngara, Pangani, Morogoro, Dodoma na Singida, Waziri ni mmoja wa watumishi wa serikali waliofanya kazi kubwa ya kupambana na Nyarubanja, mfumo wa umiliki uliokuwa ukiendeshwa Mkoa wa Ziwa Magharibi (sasa Kagera).Akiwa amesoma Shule ya Msingi Pugu na kisha kusoma Sekondari ya Minaki, ni mmoja wa Watanzania wa mwanzo waliokuwa na kazi kubwa ya kuonesha njia katika siasa za ujamaa na kujitegemea wakifuata maelekezo ya Mwalimu Julius Nyerere. Aidha, mzee huyo ambaye alishika nafasi mbalimbali katika taasisi za kisiasa katika mahojiano yake ya mwisho na waandishi wa habari waliokuwa wanatengeneza dokumentari, alisema wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere, rushwa na matumizi mabaya ya ofisi yalikuwa ni mambo yasiyovumilika.Aidha, alisema viongozi walikuwa na kazi kubwa ya kuelimisha watu kuelewa utawala maana yake nini na kushiriki katika kazi za kujenga taifa kwa uhuru na kujituma zaidi. Mzee Waziri ameacha watoto kadhaa, wajukuu na vitukuu. Miongoni mwa watoto wake ni mjasiriamali na mhamasishaji maarufu wa ujasiriamali nchini na Bara la Afrika, Maida Waziri. Aidha, Maida Waziri ni mmoja wa wanawake wanaojulikana sana katika sekta ya ujenzi nchini Tanzania akimiliki Kampuni ya Ujenzi ya Ibra Contractors.
3
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mifuko ya Jamii (SSRA) inaendelea kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa wadau na wananchi, ambayo yatasaidia kuboresha kanuni na miongozo, itakayoendelea kumnufaisha zaidi mstaafu kupitia mafao yake.Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Dk Irene Isaka alisema lengo la mamlaka hiyo ni kuendelea na maboresho ya kanuni na miongozo kwani dirisha la maoni lipo wazi kwa watanzania kuleta mawazo yao yatakayosaidia kuboresha mfumo wa mafao kwa wastaafu. “Milango ipo wazi kwa wananchi na wadau mbalimbali kuleta maoni yao ili tuweze kuboresha sheria na kanuni zinazoongoza mifuko ya jamii na kuongeza tija katika mafao ya wastaafu, alisema,” Dk Isaka.Alieleza kuwa kanuni zinazotumika sasa, zimetokana na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali wakiwemo wafanyakazi na waajiri katika kutoa maoni na mapendekezo. Maoni na mapendekezo hayo yamesaidia kupatikana kwa sheria na kanuni, ambazo zimeleta neema kwa wastaafu kwa kupata mafao stahiki na kwa wakati.“Taratibu za mafao zinampa mstaafu nafasi ya kupata mkopo katika baadhi ya benki nchini kutokana na uhakika wa pensheni yake kwa kipindi cha kustaafu kwake na kumfanya aweze kuendelea kufanya miradi mbalimbali ya maendeleo,” alisema Dk Isaka alisema tofauti na miaka ya nyuma, pensheni za wastaafu zilikuwa na ukomo wa muda wa miaka 10 mpaka miaka 12, lakini kwa kanuni za sasa pensheni ya mstaafu, atapokea kwa kipindi chote cha maisha yake ya kustaafu, hii inampa uhakika wa kupata mkopo na kuendelea kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo.“Moja ya majukumu ya SSRA ni kulinda na kutetea maslahi ya mwanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii hivyo tutaendelea kupokea maoni ili mwanachama aweze kunufaika zaidi kupitia michango yake atakapostaafu,” alisema. Alisema SSRA itaendelea kuwaelimisha wanachama na wananchi juu ya kanuni mpya ya ukokotoaji na faida zake kwa wanachama pale atakapostaafu, kwani imeonekana uelewa wa hii kanuni mpya haijawafikia watu wengi nchini na hata wale wachache waliofikiwa na taarifa hiyo wengi wao wamepotoshwa.“SSRA tumejipanga kuwafikia wanachama wote nchini na kuwapa elimu juu ya kanuni hii mpya ya ukokotoaji wa mafao ili kuwaondoa katika hofu ambayo imejengeka miongoni mwao kutokana na maneno ya baadhi ya watu wasio na uelewa wa kutosha juu ya kanuni mpya ya Ukokotoaji mafao,” alisema Dk Isaka. Alisema madhumuni ya mamlaka hiyo ni kumuondoa mstaafu katika hali mbaya ya kiuchumi baada ya kumaliza mafao yake ya mkupuo ya asilimia 25, kwa kumpatia asilimia zilizobaki kama pensheni ya kila mwezi kwa kipindi chote cha maisha yake.“Wastaafu wengi wamejikuta katika hali mbaya ya kiuchumi baada ya kupata mafao ya mkupuo na kukosa pensheni ya mwezi hivyo kwa kanuni hizi mpya zitamfanya mstaafu kusimama kiuchumi kupitia pensheni za kila mwezi,” alisema Dk Isaka. Wastaafu wengi waliofanyiwa mahojiano hivi karibuni, walionesha kuridhishwa na sheria mpya ya ukokotoaji ya mafao ya mstaafu, kwani wameeleza kuwa inatoa wigo mkubwa kwa mstaafu kuendelea na maisha yake vizuri zaidi kutokana na uhakika wa malipo ya kila mwezi.
3
['Kocha wa Chelsea Frank Lampard anataka kumsajili mchezaji wa nafasi ya ulinzi kutoka Leicester Ben Chilwell, marufuku ya kufanya uhamisho itakapokwisha, mchezaji huyo wa timu ya taifa ya England, 22 ana thamani ya pauni milioni 70 (Sun)', 'Kiuongo wa timu ya taifa ya Ufaansa, Paul Pogba, 26, anasema kuna swali wakati wote kuhusu mustakabali wake ndani ya Manchaster United (RMC - in French)', 'Barcelona wanasema winga timu ya taifa ya Brazil Philippe Coutinho hataondoka katika klabu hiyo msimu huu wa joto. (Marca)', 'Mazungumzo kati ya Barcelona na Paris St-Germain kuhusu uhamisho wa mshambuliaji Neymar yamesimama huku klabu hiyo ya Ufaransa ikiomba wachezaji watatu zaidi kufidia gharama ya mchezaji huyo. (Sport)', 'Roma bado inataka kumsajili beki wa kati wa Liverpool na timu ya taifa ya Croatia Dejan Lovren, 30. (Corriere dello Sport)', 'Wawakilishi wa kiungo wa Arsenal Mesut Ozil, 30, watasafiri kwenda Marekani kufanya mazungumzo na DC United kuhusu uhamisho wa mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ujerumani. (Express)', 'Barcelona itamruhusu Rafinha ambaye alikuwa akihusishwa na taarifa za kuhamia Liverpool na Arsenal- kuondoka kwenye klabu hiyo wakati Valencia ikiwa na mpango wa kumsajili kiungo huyo wa Brazil, 26. (Sport)', 'Kocha wa zamani wa Manchester United na Chealsea, Jose Mourinho amesema kikosi cha pili cha Manchester City kitashinda, kikiongoza moja kati ya timu zake za zamani au Arsenal. (Telegraph)', 'Kiungo wa zamani wa Tottenham na West Brom Nacer Chadli, 30, ameungana na Vincent Kompany kwenda Anderlecht kwa mkopo akitokea Monaco.(Anderlecht official website)', 'Mshambuliaji wa Bristol City Matty Taylor, 29, yuko kwenye hatua za mwisho kuhamia Oxford United. (Bristol Post)', 'Tetesi za soka Ulaya Jumapili 11.08.2019:', 'Juventus haijapoteza hamu ya kumsaini kiungo wakati wa Man United Paul Pogba, 26. (Express)', 'Pogba anasisitiza kuwa hataleta mgawanyiko miongoni mwa wachezaji licha ya madai kwamba alitaka kuondoka Trafford. (Mirror)', 'Paris St-Germain ina hamu ya kuafikia mkataba utakayoifanya Real Madrid kumnunua mshambuliaji wake raia wa Brazil Neymar, 27, kutoka kwao kwa dau la £149m mbali na klabu hiyo kuikabidhi kiungo wake wa kati raia wa Croatia Luka Modric, 33. (Times - subscription required)', 'Beki wa Tottenham Serge Aurier anataka kuondoka katika klabu hiyo huku AC Milan na klabu yake ya zamani PSG zikimmezea mate mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 raia wa Coast . (Mail)', 'Manchester United hawana hakika iwapo mlinda lango David de Gea atatia saini kandarasi mpya . Kandarsi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 inakamilika msimu ujao na raia huyo wa Uhbispania yuko hurru kuanza mazungumzo na klabu za kigeni mwezi Januari(Mirror)']
4
Na Editha Karlo-Kigoma BOTI ya mizigo iliyokuwa ikitokea Kigoma kuelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo eneo la  Kalemi imepotea katika ziwa Tanganyika ikiwa na watu sita. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu tukio hilo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdnand Mtui, alisema boti hiyo ilikuwa na shehena ya vitunguu maji magunia 110, ngano mifuko180, mafuta ya taa dumu 20 na kreti 70 za soda ambayo mpaka sasa haijulikani ilipo. Mtui alisema tukio la kupotelea ziwani boti hiyo limetokea Januari 23 mwaka huu,  saa 16:30 jioni, ambapo boti hiyo iliondoka katika bandari ndogo ya Kibirizi ikiwa na shehena hiyo ya mizigo lakini mpaka sasa haijafika Kongo na haijulikani ilipo na hakuna kilichopatikana kati ya mizigo wala abiria waliokuwa kwenye boti hiyo. Askari wanamaji wakishirikiana na Chama cha Wamiliki wa Maboti wanaendelea na utaratibu wa kuitafuta boti hiyo, inasemekana imepotelea katika maji yaliyopo Kongo. Mtui alisema kumekuwa na taarifa zilizo kuwa zikizungumzwa mitaani kwamba  kuna miili imeonekana, taarifa hizo si za kweli hadi sasa hawajajua kama watu hao watakuwa hai au wamekufa maji. "Tumewasiliana na watu walio pembezoni mwa Ziwa Tanganyika hawajaona kitu chochote hadi sasa, ninawaomba wananchi kuwa na subira wakati jitihada mbalimbali za kutafuta miili inaendelea ili waweze kuitambua,"alisema. "Baada ya kupata taarifa kuhusu  boti hiyo iliyokuwa ikielekea Kongo kwamba haijafika kwa muda uliotakiwa, Polisi kwa kushirikiana na wamiliki wa maboti walianza jitihada za kulitafuta boti hilo maeneo ya mwambao mwa Ziwa Tanganyika na hatujapata taarifa yoyote. “ Boti ingekuwa imezama mizigo iliyo kuwemo katika boti hiyo ingekuwa imeanza kuelea, tumewasiliana na  mikoa baadhi ambayo Ziwa Tanganyika limepita pamoja na nchi za Burundi na Kongo kupitia ubalozi mdogo waweze kutujulisha endapo wataiona boti hiyo," alisema Mtui. Baadhi ya ndugu wa wasafiri walio kuwemo katika boti hiyo wameanza kutandika msiba kuwaombolezea ndugu zao waliopotea katika boti hiyo , Hamisi Kakolwa ni mmoja kati ya abiria waliokuwa wakisafiri kuelekea Kalemii Kongo. Mgeni Kakolwa ni mdogo wa Hamis Kakolwa ambaye alisema ndugu yao aliondoka Januari 21 kuelekea Kalemii kupeleka biashara zake, baada ya siku mbili kupita walifanya mawasiliano na watu wa Kongo kujua kama boti waliyokuwa wakisafiria ndugu yao, wakaambiwa haijafika. Kakolwa alisema familia baada ya kuona hakuna mafanikio ya kuipata boti hiyo kwa siku saba waliamua kuandaa msiba wa kumuombolezea ndugu yao kwasababu hawana uhakika kama atakuwa amepona au amekufa.
3
KAMPALA, UGANDA MWANAMKE mmoja katika wilaya ya Hoima mashariki mwa Uganda anashikiliwa kwa madai ya kumuua mpenzi wake baada ya kumfuma akimeza dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi (ARV) Wakielezea tukio hilo, Polisi walisema kuwa, Emmanuel Tumusiime mwenye umri wa miaka 35 alishambuliwa hadi kuuawa katika makazi yake akiwa mji wa Kigorobya saa 12 jioni siku ya Jumatano wiki hii. Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la  nchini Uganda, msemaji wa polisi wa mji huo, Julius Hakiza amesema uchunguzi wa awali ulibaini kuwa Tumusiime alipigwa kichwani na shoka. ”Alipogundua kwamba mpenzi wake amefariki, mshukiwa alifunga nyumba na kupanda bodaboda hadi kwenye kituo kikuu cha polisi cha Hoima na kuripoti kesi ya mauaji,” alieleza Hakiza. Katika kituo hicho cha polisi, mwanamke huyo alikiri kumuua mpenzi wake. Mwanamke huyo anadai kuwa alijisikia uchungu sana baada ya kuhisi kuwa kuna uwezekano ameambukizwa virusi vya Ukimwi. Alikamatwa na kushikiliwa kwenye kituo kikubwa cha Hoima akishutumiwa kwa kujihusisha na mauaji. “Wapelelezi walikimbilia eneo la tukio na kulifunga kwa ajili ya uchunguzi zaidi,” alieleza Hakiza. ”Tunatoa wito kwa waathirika wa virusi vya Ukimwi mara zote kuwapa taarifa wenza wao na kuhudhuria vituo vya ushauri nasaha na kufahamu kwamba kwa kuwa mwathirika, haimaanishi ni mwisho wa maisha,” alishauri Hakiza.
2
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM MKALI wa filamu nchini na Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu ‘Wema’, amemfungulia kesi ya madai mpenzi wake wa zamani ambaye ni mwanamuziki wa bongo fleva, Nassib Abdul ‘Diamond’, kwa kumtapeli kiasi cha Sh milioni 10. Kwa mujibu wa mtandao wa Shirika la Utangazaji (BBC) idhaa ya Kiswahili, Wema aliripoti madai yake kituo cha Polisi Oysterbay akidai kuwa alimpatia mwanamuziki huyo kiasi hicho kwa makubaliano ya kazi na kuahidi kumlipa, lakini amekwenda kinyume makubaliano yao. Muhusika mkuu ambaye ni Wema alitoa maelezo kwamba watu wanamtupia lawama kutokana na hatua aliyofikia, lakini amedai kuwa amelazimika kufanya hivyo kwa kuwa yeye ndiye aliyeingia dhamana na taasisi Focus Vicoba kuchukua fedha hizo. “Naona watu wengi wananilaumu kwa kuwa nimemfungulia kesi Diamond, pasipo kuelewa kama fedha hizo pia hazikua zangu bali ni mkopo ambao niliingia dhamana katika taasisi ya utoaji mikopo ya Vicoba. “Kupitia mfuko wa Focus Vicoba nilichukua mkopo huo kwa lengo la kumpatia Diamond, ili aweze kuandaa miradi yake tena kwa makubaliano kuwa atazirudisha ili tuweze kufanya marejesho ya mkopo tuliochukua,” alisema Wema. Mrembo huyo alieleza muda waliiopeana ahadi ya kurudisha fedha hizo umepita na Diamond haoneshi dalili ya kuzirejesha wakati wanatakiwa kuzirudisha kwa wakati . “Yote haya yasingenikuta, lakini sina jinsi kwani natakiwa kurudisha pesa za watu nimekuwa nikimpigia simu Diamond hataki kupokea simu zangu, lakini kama alitaka kunidhulumu ni bora angejiunga mwenyewe na hawa Vicoba ili apate mkopo na kufanya mambo yake au kama aliona hawezi kwa kujishtukia basi angetumia ile tovuti yao, angepata kwa urahisi na hakuna mtu yeyote angejua kama amekopa ila sio kukimbia kulipa deni la watu,” alisema. Hata hivyo Diamond ambae kwa sasa yupo nchini Burundi kwa ajili ya ziara yake kimuziki, tayari ametumiwa taarifa na jeshi la polisi kwa barua ya wito kufika kituoni pindi atakaporejea nchini, huku mama yake mzazi akifikishiwa ujumbe huo nyumbani kwake. Wema ambae alimwekea dhamana, yupo katika kipindi kigumu ambacho kinaweza kupelekea kufilisiwa mali zake ambazo aliziandikisha wakati wa kuchukua mkopo huo ili ziweze kufidia deni hilo. Kwa mujibu wa kiongozi wa taasisi hiyo ambae aligoma kutajwa jina lake gazetini, alisema kuwa ni kweli Wema alifika katika ofisi zao zilizopo Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, ili apewe muongozo lakini alipotakiwa kufuata taratibu za kiofisi kama wanachama wengine wanavyofanya katika vikundi, hakukubaliana na utaratibu, hivyo kushauriwa ajiunge kupitia tovuti . MTANZANIA ilimtafuta Meneja wa Wema, Martin Kadinda, ambae alieleza hajui chochote kuhusu kufungulia kwa kesi hiyo, akaomba apewe muda kumtafuta msanii huyo ili aweze kupata ufafanuzi juu ya suala hilo, lakini hakueleza nini kilichojiri na kusisitiza asubiriwe. Gazeti hili halikuishia hapo, lilimsaka Meneja wa Diamond, Babu Tale, ambae alionekana kushtushwa na habari hizo na kudai kuwa hazina ukweli wowote.
1
MASHINDANO ya Vijana waliochini ya umri wa miaka 17 kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati (Cecafa U-17) yanatarajiwa kuanza leo jijini Dar es Salaam kwa kushirikisha timu 10 katika Uwanja wa Taifa na Chamazi.Serengeti Boys atafungua dimba kwa kucheza dhidi ya Burundi katika mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10:00 jioni na kufuatiwa na Rwanda dhidi ya Sudan kuanzia saa 2:00 usiku kwenye uwanja huohuo.Mashindano hayo makubwa ya Cecafa kwa ukanda huu kwa umri huo, mshindi wake ndio ataungana na timu ya Tanzania, Serengeti Boys kuwakilisha kanda hiyo katika fainali za Afrika za Vijana (Afcon U-17), ambazo zinatarajiwa kufanyika nchini mwakani.Kama Serengeti Boys itatetea ubingwa wake, basi mshindi wa pili ndiye atafuzu kucheza fainali hizo za vijana zitakazofanyika mwakani nchini Tanzania, ambazo zitamalizika Agosti 26.Nchi zinazoshiriki mashindano hayo ni wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Somalia, Sudan, Sudan Kusini, Ethiopia, Djibouti, Rwanda na Burundi. Tanzania ikiwa mwenyeji, timu yake ya Vijana ya Serengeti Boys inaingia ikiwa na matumaini ya kutetea ubingwa iliyoutwaa Aprili mwaka huu, nchini Burundi baada ya kuifunga Somalia mabao 2-0.Tanzania ipo Kundi A lenya timu za Rwanda, Burundi, Somalia na Sudan na Kundi B lina timu za Uganda, Kenya, Ethiopia, Sudan Kusini na Djibouti na itafungua dimba kwa kucheza na Burundi katika Uwanja wa Taifa jioni ukitanguliwa na mchezo dhidi yaRwanda na Sudan utakaochezwa mchana.Kocha wa Serengeti Boys, Oscar Mirambo alisema jana Serengeti Boys wamejiandaa, wana ari na wanacheza mbele ya mashabiki wao, hivyo wana kila sababu ya kushinda mchezo huo ili waweze kutetea ubingwa, kwani tayari wameshakata tiketi ya kucheza fainali za Afcon mwakani. “Wachezaji wamejiandaa na wameniahidi ushindi katika mchezo wa kesho (leo) kikubwa mashabiki waje kwa wingi kuishangilia timu yao,” alisema Oscar.Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka la Tanzania, TFF, Wilfred Kidao alisema kikosi cha Serengeti Boys kitafanya vizuri kwenye michuano hiyo ambayo ni maalumu kwa ukanda wa Cecafa kupata mwakilishi wa Afcon U-17.Kidao alisema michuano hii inafanyika katika kanda mbalimbali ili kupata timu saba zitakazoshiriki michuano ya Afcon U-17, 2019. ‘’Timu ipo kambini katika Uwanja wa Azam Complex na imecheza michezo ya kirafi ki na timu za vijana chini ya miaka 20 ya Simba, Azam, Cosmo na nyingine za Daraja la Kwanza na imeshinda mechi zote, ’’ alisema Kidao.Kidao amewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi kuipa nguvu timu yao kwani mashindano hayo yatakuwa hayana kiingilio. Kikosi cha Serengeti Boys ni Shaban Kimwaga, Mwinyi Abdallah ,Alphonce Mabula, Bernard Pastory ,Paschal Msindo, Salim Lupepo ,Ally Hamis ,Lenox Chance, Amiri Njeru, Mustapha Daniel Jefferson Thomas ,Morice Michael ,Keffa James, Said zanda, Ladaki Juma, Edison Mshirakandi, Jaffar Mtoo, Agiri Ngoda ,Kelvin Pius na Salum Milinge.
4
BUJUMBULA, BURUNDI MAHAKAMA ya Burundi imemuhukumu kifungo cha miaka mitano jela mwalimu mkuu ambaye alikamatwa hivi karibuni akimfanyia mtihani wa taifa mwanafunzi. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), mbali na kifungo hicho, mahakama hiyo pia imemfungia mwalimu huyo, Benjamin Manirambona kutojihusisha na shuhghuli yoyote ya kufundisha ama kuajiriwa katika ofisi ya umma kwa kipindi cha miaka 10. Mwalimu huyo alikamatwa Ijumaa wiki iliyopita na polisi aliyekuwa aliyeingia katika chumba cha kufanyia mtihani akiwa amevaa sare za wanafunzi. Baada ya kukamatwa, mwalimu huyo wa Chuo cha Ufundi cha Butere kilichopo mjini hapa, alikiri makosa na akasema alikuwa akimfanyia mtihani ofisa mmoja wa jeshi ambaye anafanya kazi ya kulinda amani nchini Somalia. Katika maelezo hayo, mtuhumiwa huyo alisema ofisa huyo alikuwa akihitaji ufaulu wa juu ili aweze kujiunga na Chuo Kikuu. Alisema mwanajeshi huyo alimuahidi malipo wakati atakaporejea akitokea Somalia. Hata hivyo, Waziri wa Elimu, Janvière Ndirahisha, ambaye aliwasili eneo la tukio akiwa na askari waliokuwa wamevaa sare, aliyakataa maelezo ya   Manirambona akisema ni ya uongo. “Kila kitu ambacho unakizungumza ni cha uongo, kwahiyo tunakuchukua na tutakuchunguza kwa jinsi tulivyosikia sio mara ya kwanza kufanya hivyo,” alieleza waziri huyo. Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo ni mhasibu wa chuo hicho, Eric Nkurunziza na mwalimu Lazard Nihezagire, ambao wamehukumiwa kifungo cha miaka miwili na kufungiwa kufanya kazi katika ofisi za umma kwa muda wa miaka mitano.
2
NA OSCAR ASSENGA- LUSHOTO WATU wawili wa familia moja, mke na mume wakazi wa Kijiji cha Baga. Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, wamefariki dunia baada ya kunywa chai ya rangi inayodhaniwa kuwa na sumu. Mbali ya hilo, mpwa wao amenusurika katika tukio hilo ambalo limeacha maswali mengi. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, alithibitisha kutokea tukio hilo. Alisema lilitokea Juni 19, mwaka huu saa saba mchana wakati familia hiyo ilipoandaa kinywaji hicho. Aliwataja waliofariki wakati wakipatiwa matibabu katika Zahanati ya Baga kuwa ni Rajabu Ally (73) na Amina Rajabu (62). Kamanda Wakulyamba alisema katika tukio hilo, mpwa wao Adam Saidi (12), mwanafunzi wa darasa la tatu  Shule ya Msingi Mashine, alinusurika kifo. Alisema miili ya marehemu imefanyiwa uchunguzi wa awali na kukabidhiwa ndugu kwa taratibu za mazishi, huku Jeshi la Polisi likiendelea na upelelezi wa tukio hilo. “Katika tukio hilo ambalo limepoteza watu wa familia moja, mpwa wao alinusurika baada ya kunywa chai idhaniwayo kuwa ni yenye sumu, tunaendelea na upelelezi wa tukio hili,” alisema Kamanda Wakulyamba.
3
ISLAMABAD, PAKISTAN WAZIRI Mkuu wa Pakistan Imran Khan amesema kuwa haitoruhusu genge lolote la kigaidi kuendesha shughuli zake nchini humo na kusisitiza kuwa nchi hiyo sio makazi ya magaidi. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA limesema kuwa Imran Khan amesema hayo mbele ya wafuasi wake kusini mwa Pakistan na kuongeza kuwa, serikali yake haitowaruhusu magaidi kutumia ardhi ya nchi hiyo kushambulia nchi jirani. Matamshi hayo ya Waziri Mkuu wa Pakistan yamekuja siku chache tangu ulipopamba moto mzozo baina ya nchi hiyo na India kutokana na mashambulizi ya kigaidi yaliyowalenga wanajeshi wa India. Mzozo mpya katika uhusiano wa Pakistan na India ulizuka baada ya kundi la kigaidi linalojiita Jaish al Muhammad kushambulia wanajeshi wa India huko Kashmir tarehe 14 mwezi ulioisha wa Februari na kuua wanajeshi 44. Jeshi la India lilituma ndege zake na kushambulia baadhi ya maeneo ndani ya ardhi ya Pakistan likidai kuwa ni maficho ya magaidi hao. Pakistan nayo ilijibu mashambulizi hayo ya India kwa kutungua ndege mbili za nchi hiyo na kumteka nyara rubani mmoja wa India ingawa baadaye ilimuachilia huru ili kuonesha nia yake njema. Siku moja kabla ya kushambuliwa wanajeshi wa India basi lililokuwa limebeba walinzi wa mpakani wa Iran lilishambuliwa huko Zahedan, makao makuu ya mkoa wa Sistan na Baluchistan wa Iran unaopakana na Pakistan na kusababisha maafisa 27 wa Iran kuuawa na wengine 13 kujeruhiwa. Kundi la kigaidi la Jaish al Dhulm linaloendesha shughuli zake katika ardhi ya Pakistan lilijigamba kuhusika na shambulio hilo.
2
NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM SERIKALI imesema inafuatilia kwa karibu mlipuko wa ugonjwa wa Marburg uliogundulika nchini Uganda na kuchukua hatua mbalimbali kuudhibiti usiingie nchini. Ili kukabiliana nao, Serikali imenunua na kusambaza mashine maalumu za kupima joto la mwili wa binadamu ikiwa ni hatua mojawapo ya kudhibiti ugonjwa huo. Akizungumza na MTANZANIA jana ofisini kwake, Mratibu wa Vituo vya Afya Mipakani wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Remidius Kakulu alisema mashine 12 zimeongezwa na kusambazwa katika maeneo ya bandarini, mipakani na kwenye viwanja vya ndege. Aliyataja maeneo hayo kuwa ni viwanja vya ndege vya Julius Nyerere (JNIA), Kigoma, Songwe,  Bandari ya Dar es Salaam na Bandari ya Tanga. “Katika Uwanja wa JNIA na Kigoma awali kulikuwa na mashine lakini kwa kutambua umuhimu wa suala hili tumelazimika kuongeza mashine nyingine ili kuimarisha ukaguzi.   “Mashine hizo pia zimefungwa katika Bandari ya Kigoma, Uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) na Uwanja wa ndege wa Mwanza,” alisisitiza.   Aidha Kakulu aliyataja maeneo mengine ambako mashine hizo zimesambazwa kuwa ni pamoja na Mpaka wa Mtukula, Horohoro, Kasumulu, Sirari, Murongo, Tunduma, Namanga, Tarakea na Tunduma.   Meneja Kitengo cha Uratibu wa Milipuko ya Magonjwa na Majanga wa Wizara hiyo, Dk. Ali Nyanga alisema hadi sasa hakuna mtu yeyote aliyegundulika nchini kuwa na ugonjwa huo.  
3
Na MWANDISHI WETU- NZEGA MWENYEKITI wa Taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation inayoshughulikia utawala bora na haki, Khamis Mgeja, amemshangaa Rais Dk. John Magufuli kwa kutoshiriki kuaga miili ya askari polisi waliouawa na majambazi, Kibiti mkoani Pwani wiki iliyopita. Amesema kama Rais Magufuli angeshiriki kuaga miili hiyo akiwa na askari polisi na familia za marehemu, angeonyesha ni kwa jinsi gani alivyoguswa na mauaji hayo ya kikatili. Mgeja aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora akiwa njiani kuelekea Shinyanga. “Pamoja na kwamba siku miili hiyo ilipokuwa ikiagwa Rais alikuwa kwenye ufunguzi wa hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa makazi ya wananchi pale Magomeni, Dar es Salaam, ukweli utabaki palepale, kwamba alitakiwa kuahirisha shughuli hizo ili akashiriki kuaga miili ya Watanzania hao. “Washauri wake wangemshauri juu ya hilo kwani uzito wa tukio la kuuawa kwa askari wetu, ulikuwa wa aina yake na hauwezi kulinganishwa na tukio la kufungua hosteli na nyumba za makazi. “Kwa hiyo, naamini siku hiyo Rais angetumia busara tu kuhairisha shughuli nyingine ili akawaage askari hao kwa sababu waliuawa wakati wakitimiza majukumu yao ya ujenzi wa taifa na kulinda raia na mali zao. “Nasema hivyo kwa sababu Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kutwambia kwamba kupanga ni kuchagua, kwa hiyo, siku hiyo Rais alitakiwa kwenda kuaga miili hiyo kwa sababu ya umuhimu wa tukio lenyewe. “Pamoja na Rais kutoshiriki tukio hilo, viongozi wengi wa Serikali hawakuwapo kwani walikuwa wamekwenda kushiriki matukio ya rais,” alisema Mgeja. Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, aliongoza waombolezaji kuaga miili ya askari hao. Wiki iliyopita, watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, waliwaua kwa risasi askari wanane mkoani Pwani walipokuwa wakitoka kufanya doria.
3
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM MATUMIZI ya zebaki katika uchimbaji wa madini  umeelezwa kuwa hatarishi kwa afya ya binadamu  hasa kwa watumiaji ambao ni wachimbaji wadogo wa madini pamoja na mazingira yanayoizunguka eneo husika. Akizungumza wakati wa kufunga maadhimisho ya Siku tatu ya miaka 50 ya taaluma ya Jiolojia  mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Waziri wa Madini, Doto Biteko, alisema wizara imeingia mkataba unaozuia matumizi ya zebaki duniani kwani  ni kemikali ambayo si rafiki kwa afya ya mwanadamu pamoja na Mazingira yanayozunguka. “Saidieni katika kuhakikisha umoja wenu unasaidia taifa hasa katika kutunza rasilimali zetu. Tuungane na serikali kuhakikisha madini yetu yanachimbwa kihalali huku tukizingatia usalama wa wachimbaji, watu wanaowazunguka na mazingira kwa ujumla ili kuleta tija kwa nchi yetu,” alisema. Alisema jiolojia ni moja ya taaluma inayogusa karibia nyanja zote za maisha na kuwaomba wanajiolojia kushirikiana na serikali katika kuhakikisha mbadala wa zebaki unasisitizwa kama njia moja wapo ya kupunguza athari ambazo zingepelekea uharibifu wa mazingira. Waziri Biteko alisema taaluma ya jiolojia ni muhimu sana hasa katika sekta ya madini kwani  sekta  hiyo  ni muhimu kwa ajili ya uchumi wa nchi  hivyo kuna kila sababu ya wanajiolojia kufanya kazi zao kikamilifu na kuunga mkono azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujenga Uchumi wa Kati na viwanda ifikapo 2025. “Nendeni mkawe chachu ya mabadiliko ya sekta hii kwa manufaa ya nchi yetu na sio kwa manufaa binafsi. Mkawe waaminifu katika kazi zenu bila hivyo mtakua mnakwamisha watanzania wenzenu hasa wale wanaojipinda kuhakikisha wanapata mitaji ya kuwawezesha kufanya uchimbaji wa madini kikamilifu,” alisema Biteko. Aidha alisema NEMC watatangaza kipindi cha mpito juu ya matumizi ya Zebaki na kuwataka wadau kutoa ushirikiano stahiki. Naye Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dk. Samuel Gwamaka alisema matumizi ya zebaki katika uchimbaji wa madini ni hatari kiafya na serikali haiwezi kuacha watu wake wakapoteza maisha kwasababu yakupata faida. Alisema  serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dk. John Magufuli ina lengo la kuwafanya wachimbaji wadogo kukua na kuwa wachimbaji wakubwa.
3
Na MWANDISHI WETU- DAR ES SALAAM MAZAO ya nafaka yakiwamo mahindi, mpunga, mtama na uwele ndio mazao makuu ya chakula ambayo hutumiwa na Watanzania wengi waishio maeneo ya mijini na vijijini. Jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanywa na Serikali kuongeza tija kwa mazao hayo ambayo huhifadhiwa kwa muda mrefu zaidi kuliko mazao mengine ya chakula, ambapo uzalishaji wake umefikia wastani wa tani milioni 3,897,500 kwa mwaka. Inaelezwa kuwa pamoja na ongezeko la uzalishaji, teknolojia zinazotumika katika uvunaji, utayarishaji na hifadhi ni duni na husababisha upotevu mkubwa wa mazao hayo, ambapo wastani wa tani 1559,000 za mazao ya nafaka  hupotea kila mwaka nchini. Ili kukabiliana na changamoto hizo, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imekamilisha kuandaa mkakati wa Taifa wa hifadhi ya mazao kwa lengo la kuwa na dira ya kupunguza upotevu unaojitokeza katika mazao ya chakula nchini. Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya mwaka 2017/18, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tzeba, anasema Serikali imechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto ya hali ya usalama wa chakula ikiwamo upotevu wa mazao kabla na baada ya mavuno na sumukuvu. Anasema katika kuimarisha ubora na usalama wa mazao ya chakula nchini, Wizara kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) II, itajenga makaushio ya kisasa 30 na kusambaza vifaa vya kukaushia kwa wakulima wa nafaka katika halmashauri za Sikonge, Chemba, Kondoa, Chamwino, Kiteto na Manispaa ya Dodoma kwa lengo la kudhibiti sumukuvu na madhara yake. Anaongeza kuwa katika kuhakikisha mazao ya wakulima yanaongezewa thamani na kuwa na soko zuri, Wizara kupitia Programu ya ASDP II itajenga maghala manne yenye uwezo wa kuhifadhi tani 1,000 katika mikoa ya Singida (Mahindi), Mwanza (Mpunga), Kigoma (Mahindi) na Manyara (Mahindi). Dk. Tizeba anasema Wizara itakamilisha ujenzi wa masoko na maghala 45 ya kimkakati katika mipaka ya Mulongo, Sirari, Kabanga, Kahama na Kyerwa-Nkwenda ili kuleta ufanisi katika biashara za mipakani na kudhibiti wafanyabiashara kutoka nje ya nchi kuingia moja kwa moja mashambani na kununua mazao ya wakulima kwa bei ndogo. Kwa mujibu wa Dk. Tizeba, kupitia mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa mpunga, Serikali imekusudia kujenga maghala matano (5) yenye uwezo wa kuhifadhi tani 8,400 katika skimu za umwagiliaji za Njage (tani 1,700), Msolwa Ujamaa (tani 3,400), Mvumi (tani 1,300), Kigugu (tani 1,000) na Mbogo Komtonga (tani 1,000). Aidha, Dk. Tizeba anasema Wizara kupitia Programu ya ASDP II itakamilisha ujenzi/ukarabati wa maghala 33 katika wilaya za Iringa, Njombe, Nsimbo, Mlele na Songea kwa ajili ya hifadhi ya mahindi, ambapo wakulima watahifadhi na kuuza mazao yao kwa pamoja na kujengewa uwezo kuhusu umuhimu na uendeshaji wa ushirika. Kuhusu sumukuvu, anasema katika mwaka 2016/17 Serikali kupitia Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko imenunua tani 3,300.04 za mahindi kutoka kwa wakulima wa mikoa ya Iringa, Njombe na Ruvuma na kuongeza thamani ya zao kwa kusagisha tani 1,047.8 za mahindi. Kupitia Programu ya ASDP imeweka vifaa vya kutunza ubora wa nafaka katika maghala 79 yanayohifadhi mahindi katika mikoa ya Rukwa–Halmashauri ya Kalambo (9), Ruvuma–Songea Vijijini (20), Songwe–Mbozi Vijijini (20), Mbeya–Mbeya Vijijini (13), Iringa–Mufindi (10), Njombe – Njombe Vijijini (7). Akifafanua zaidi, Dk. Tizeba anasema katika kuongeza thamani ya mazao Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kupitia Mradi wa Sera na Maendeleo ya Rasilimali Watu, imenunua mashine 14 za kusindika mpunga katika skimu za Mombo Kivulini, Mawemairo, Ipatagwa, Ituro na Mbuyuni, Lekitatu, Mkula, Musa Mwinjanga, Nakahuga, Magozi, Kilangali, Mkindo na BIDP. Waziri Tizeba anasema Wizara yake pia imefanya tathmini katika halmashauri za mikoa 12 ya Mwanza, Simiyu, Geita, Tabora, Kigoma, Shinyanga, Dodoma, Tanga, Morogoro, Kilombero, Arusha na ili kufahamu mahitaji ya ukarabati; ujenzi wa maghala mapya kwa ajili ya hifadhi ya mazao ya mpunga na mahindi. Kuhusu sumukuvu, Dk. Tizeba anasema Serikali imechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na tatizo hilo ikiwamo kuandaa andiko lililowasilishwa FAO na kupata ufadhili wa kudhibiti sumukuvu ambapo jumla ya Dola za Marekani 151,000 sawa na Sh milioni 300 zimetolewa na utekelezaji tayari umeanza. Aidha, Serikali imelenga kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kupitia viwanda. Hata hivyo, ili kufikia malengo hayo ni lazima kuimarisha uzalishaji wa mazao ya kilimo ambayo ndiyo yatakuwa malighafi katika viwanda vinavyotarajiwa kujengwa.
3
WAKATI serikali ikiendelea na ujenzi wa reli ya kisasa kati ya Dar es Salaam na Mwanza yenye urefu wa kilometa 1,219 na pia kukarabati ile ya zamani maarufu kama `Reli ya Kati’, Shirika la Reli Tanzania (TRL), limetangaza kugeukia ujenzi wa reli za mijini, ikianza na Dar es Salaam na Dodoma.Lengo la reli hizo, limetajwa kuwa ni kuondoa msongamano katika maeneo ya mijini, lakini pia kuziunga sehemu zenye shughuli kuu za kiuchumi kama viwanda, ili kuweza kusafirisha bidhaa kwa urahisi.Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa alipokuwa anazungumzia mikakati mbalimbali ya kuimarisha usafiri wa reli nchini. Alisema kwa Dar es Salaam, mbali ya kuimarisha safari za sasa za ndani ya Dar es Salaam na maeneo jirani kama Pugu, zitajengwa pia reli mpya kati ya Mbezi na Bagamoyo, nyingine itakwenda Mbagala, lakini itakuwepo pia ya kwenda Uwanja wa Ndege.“Mpango huu wa kuwa na mtandao mpana wa reli za mijini unalenga kukabiliana na foleni, hasa ikizingatiwa katika miji na majiji kunakuwa na watu wengi, hivyo kukwamisha katika shughuli zao na foleni.“Ndiyo maana tunaangalia uwezekano wa kuwa na mtandao wa reli, tukianza na Dar es Salaam na Dodoma. Haya mambo yapo katika mipango kwa muda mrefu, ila kwa sasa tunakwenda kutenda. Ni suala la muda tu,” alisema Kadogosa ambaye ofisi yake inajiandaa kufyatua jingo la ghorofa saba eneo la Ihumwa, jirani na mji mkuu wa kiserikali wa Dodoma.Aliongeza kuwa reli hizo zitasaidia pia usafirishaji wa bidhaa kutoka viwandani, kwani zitakuwepo pia zitakazoungwa na viwanda ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na malighafi. Tayari Dar es Salaam kuna safari za treni za ndani ya jiji, ya Tazara- Pugu-Mwakanga, ya Stesheni ya Dar es Salaam-Pugu na Stesheni ya Dar es Salaam-Ubungo, ambazo zimetajwa kusaidia wakazi wake kutumia muda mfupi wa safari tofauti na mabasi ya abiria.Aidha, kwa kutumia usafiri wa treni, abiria wengi wamekuwa wakisafirishwa kwa wakati mmoja. Mathalani, kwa safari moja, treni kati ya Stesheni-Pugu husafirisha zaidi ya abiria 2,000 kutokana na mabehewa yake kati ya 19 na 23. Behewa moja hubeba abiria kati ya 80 na 120 na safari huchukua kati ya nusu saa na saa moja, wakati kwa safari kama hiyo kwa basi, abiria huweza kutumia hata saa 3-4.
3
Mwandishi Wetu -Dodoma MRADI wa kuendeleza zao la mtama nchini wa kampuni ya Bia ya TBL Plc, unaendelea kunufaisha wakulima wa zao hilo mkoani Dodoma, ambapo wanapatiwa mbegu za kisasa, mbinu za kuendesha kilimo cha kisasa kinachofanikisha kuongezeka kwa mavuno pia wanakuwa na uhakika wa kuuza mavuno yao kwa kampuni hiyo. Akizungumza n kwa niaba ya wakulima wenzake katika mahojiano yaliyofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni, Issa Dinya,  alisema kutokana na mradi huo wameanza kulima zao la mtama kibiashara kwa kuwa wana uhakika wa soko tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo walilima zao jilo kwa ajili ya matumizi ya chakula. Kupitia mradi huo wa majaribio unaoendeshwa kwa ushirikiano wa TBL Plc, WFP na FtMAumenufaisha zaidi ya wakulima wadogo 2,000 ambao mavuno yao yaameongezeka kwa asilimia 77 na maisha yao kuwa bora, mkakati wa kampuni ni kuinua wakulima wadogo kupitia kununua mazao yao kwa bei nzuri kwa ajili ya malighafi za kuzalisha biadhaa zake. Mradi huo wa ushirikiano ulianza mwezi Januari Mwaka 2020 ambapo TBL Plc, Ilikubaliana na wakulima kununua zao lao la mtama mkoani Dodoma na Manyara, ambapo taasisi za WFP na FtMA zimewezesha wakulima kupata mbegu za mtama, bima, ushauri wa kilimo cha kitaalamu na uhakika wa masoko. Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Plc, Philip Redman, alisema anafurahia kuona mafanikio ya mradi huo wa mtama kwa kuwa umeenda sambamba na mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha kilimo cha mtama nchini Tanzania na kuwezesha wakulima wa zao hilo kuendelea kuwa na kipato cha uhakika kuanzia sasa na katika siku za mbele.  “Mkakati wetu wa kununua malighafi ni mkakati wetu mojawapo wa kuchangia jitihada za Serikali za kukuza uchumi wa nchi,” alisema Redman. Akiongea katika moja ya mikutano ya uhamasishaji wa kilimo cha mtama mkoani Dodoma karibuni, Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa, Mustapha Yusuf, aliipongeza TBL kwa mkakati wake wa kununua malighafi kutoka kwa wakulima nchini. “Mkakati huu kwa kiasi kikubwa umeleta hamasa kwa wakulima kuzalisha zao la mtama kibiashara nchini na utawanufaisha kwa kuboresha maisha yao sambamba na kupata mbegu bora ambazo zinafanikisha kuzalisha mtama wenye kiwango kizuri na mavuno yao kuongezeka,” alisema
5
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema linaendelea kufanya uchunguzi dhidi ya tukio la utekaji kwa msaidizi wa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, Allan Kiluvya, ili kubaini undani wa tukio hilo kabla ya kutoa taarifa rasmi juu ya suala hilo.Akizungumza Dar es Salaam Kamanda wa Kanda hiyo Lazaro Mambosasa amesema kimsingi tukio hilo linahitaji upelelezi wa kutosha ili kubaini kilichotokea, kutokana na kuwa na mazingira yanayotoa picha tofauti na hivyo kusababisha shaka.“Tunaendelea na uchunguzi ili kubaini kitu kinachodaiwa kwamba mhusika alitekwa, ukiangalia clip baba mzazi alisema mtoto alipigwa sana, lakini mtoto aliposimama alisema ni mzima wa afya hajapigwa na hajateswa, lakini ukienda zaidi watekaji wamshushe wapi, wamshushe karibu na nyumbani kwa hiyo wanaongea lugha moja, mtu aliyekuteka hawezi kukushusha nyumbani,” amesema Mambosasa.Alisema tukio hilo halina tofauti na tukio la aliyekuwa msaidizi wa Zitto Kabwe, ambaye taarifa zilisema mtu huyo alikwenda kushushwa kwa shangazi yake.Alisisitiza kuwa kwa ujumla matukio yote hayo yanaleta shaka, hivyo kuashiria kuwa kuna ‘michezo’ ya baadhi ya watu inayohusiana na matukio hayo.Alisema kama kweli watu hao walitekwa, upelelezi wa polisi unaoendelea, utabaini ukweli wa matukio hayo, ambayo kimsingi yanaleta shaka kutokana na kuwa na kasoro mbalimbali, zinazomfanya mtu ajiulize mara mbilimbili.
3
NA ALLAN VICENT, Tabora  KANISA la Free Pentecoste (FPTC) Kituo cha Ipilili wilayani Nzega mkoani Tabora, limetoa msaada wa mavazi yenye thamani ya Sh 650,000 kwa wakoma wanaolelewa katika Kijiji cha Iduguta wilayani hapa. Mchungaji wa kanisa hilo, Jonas Msubi, alisema wametoa msaada huo ili kuonesha moyo wa upendo na kuwapunguzia changamoto za ukosefu wa mavazi watu hao. Alisema msaada huo umetolewa na waumini hao kwa kuchanga kidogo kidogo ili waweze kutoa sadaka kwa wenzao wenye uhitaji waliopo katika kijiji hicho. Alisema wataendeleza moyo huo wa kujitolea kusaidia jamii zenye mahitaji katika wilaya hiyo na maeneo mengine yenye watu wenye uhitaji kama hao. Mariamu Joshua na Angelina Musa ni miongoni mwa watu wenye ukoma katika kituo hicho ambao walipata msaada huo, ambapo kwa nyakati tofauti walisema walikuwa na uhaba wa mavazi hivyo wanashukuru kanisa kwa kuguswa kuwasaidia. “Tunawashukuru sana waumini wa kanisa hilo kwa moyo wao wa upendo, msaada huo utatusaidia sana kwani wengi wetu tulikuwa na uhaba wa mavazi,” alisema Angelina. Alisema kwa sasa wana changamoto ya chakula hasa mahindi kwa kuwa mwaka huu mvua zimenyesha sana hivyo kuambulia mpunga tu hivyo waliomba jamii kuwasaidia mahindi ili kukidhi mahitaji yao ya chakula. Awali akipokea msaada huo, Mchungaji Yusufu Sarangi wa misheni ya Iduguta, alilishukuru kanisa hilo kwa msaada huo wa nguo na kuongeza kuwa wasichoke kuwasaidia kwa kile watakachojaliwa ikiwemo chakula. Kwa upande wa Mchungaji Msubi aliahidi kanisa lake litaangalia uwezekano wa kuwasaidia mahindi kama walivyoomba huku akisisitiza kuwa lengo lao ni kuendelea kudumisha umoja kati ya waumini wao na watu wenye mahitaji.
3
Wafanyabiashara hao wamesema, pamoja na maafa makubwa waliyoyapata hawajaona viongozi wakuu wa serikali wakafika kuwafariji.Aidha wamesema, wanahitaji muda zaidi wa kulipa madeni yao.Hata hivyo mfanyabiashara mwingine Lucas Mushi alisema wameweza kuwasiliana na taasisi walizokopa fedha kuwaeleza hali halisi na wameambiwa wasubiri watajibiwa.Alisema katika mazingira yao magumu wameomba kupewa muda wa nyongeza wa kurejesha mkopo na pia kuangaliwa kama inawezekana waweze kupewa mikopo mingine ili waweze kuinuka tena kibiashara.Pia alisema wanashindwa kuelewa ni nini msimamo wa Serikali juu ya soko hilo kwa sababu viongozi wana kauli tofauti juu ya soko hilo.Aidha alisema hata kama Serikali ilikuwa na mpango wa kuboresha soko hilo basi wangefanya hivyo kabla wafanyabiashara hawajajenga kwa fedha zao au watoe miaka kadhaa ili wafanye biashara kurejesha hali yao ya awali ya biashara ndipo ujenzi mwingine ufanyike.Kwa upande wa Mwenyekiti wa soko hilo la Mchikichini, Jumanne Kongogo, alisema hasara iliyopatikana ndio inasababisha malalamiko yote hayo.
5
NA BADI MCHOMOLO, MICHUANO ya kimataifa ya Olimpiki inaendelea kutimua vumbi jijini Rio de Janeiro nchini Brazil, huku michuano hiyo ikitarajia kufikia tamati mwishoni mwa wiki hii Agosti 21, ambapo itakuwa siku ya Jumapili. Hadi sasa Marekani inaongoza kwa kukusanya medali nyingi kutokana na wawakilishi wake kufanya vizuri dhidi ya mataifa mengine, hata hivyo inadaiwa kwamba nchini hiyo inafanya vizuri kutokana na idadi kubwa ya washiriki ambao wana uwezo mkubwa. Kuna mataifa mengine hadi sasa yameshindwa kufanya vizuri na kukosa kabisa tuzo. Hii inatokana na washiriki wake kuwa wachache, hivyo kuwafanya washindane kwenye michezo michache. Hata hivyo, mbali na mataifa kuonesha ubora wao katika michuano hiyo, kuna baadhi ya wanamichezo walipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri kutokana na ubora wao lakini wamekuwa wa kwanza kuyaaga. SPOTIKIKI leo hii imekuchambulia wanamichezo ambao walipewa nafasi lakini wamekuwa wa kwanza kuaga. Novak Djokovic Huyo ni bingwa wa michuano ya mchezo wa tenisi kutoka nchini Serbia, anashika nafasi ya kwanza kwa ubora katika mchezo huo duniani kwa upande wa wanaume. Nyota huyo alipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika michuano hiyo, lakini alishangaza wengi baada ya kuyaaga mashindano hayo ambayo yanafanyika mara moja kwa miaka minne. Djokovic alikuwa alijikuta akibubujika machozi kwenye raundi ya kwanza kwenye Olimpiki baada ya kushindwa kuonesha ubora wake dhidi ya Juan Martin Del Potro, raia wa nchini Argentina ambaye anashika nafasi ya 141 kwa ubora katika mchezo huo duniani. Djokovic alipewa nafasi ya kufanya vizuri kutokana kushindwa kufanya hivyo kwenye michuano ya Wimbledon. Hata hivyo baada ya kushindwa kwenye Wimbledon mwezi mmoja uliopita alishindwa kushiriki michuano ya Roger Cup kwa ajili ya kujiandaa na Olimpiki, lakini hata hivyo alifungasha virago mapema kwa kufungwa setti 7-6 (7-4) 7-6 (7-2). Huyu ni bingwa mtetezi wa tenisi kwa upande wa wanawake kwenye michuano ya Olimpiki, alifanya vizuri mwaka 2012 jijini London, lakini mwaka huu ameshindwa kutetea ubingwa wake na kujikuta akitolewa mapema kwenye michuano hiyo dhidi ya Elina Sitoniva kutoka nchini Ukraine. Serena mbali na kuwa bingwa wa mchezo huo mwaka 2012, lakini mwaka huu alionesha uwezo wake kwenye michuano ya Wimbledon na kutwaa ubingwa, lakini kwenye Olimpiki ametolewa mapema. Nyota huyo alitolewa kwa seti 6-4-6-3 dhidi ya bingwa huyo ambaye anashika nafasi ya 20 kwa ubora wa mchezo huo duniani. Hata hivyo, mbali na kutolewa kwa mchezaji mmoja mmoja, lakini Serena hakufanya vizuri na dada yake Venus Williams kwenye michuano hiyo huku wakiwa kama timu, ambapo napo walitolewa mapema dhidi ya timu kutoka Jamhuri ya Czech. Andy Murray Alifanya vizuri kwenye michuano ya Wimbledon mwaka huu na kuchukua taji la michuano hiyo. Kutokana na kile ambacho alikifanya kwenye michuano hiyo kila mmoja alimpa nafasi ya kufanya hivyo kwenye Olimpiki, hasa kutokana na kushika nafasi ya pili kwa ubora duniani. Hali ilikuwa tofauti na ushindani mkubwa aliokutana nao kwenye michuano hiyo ilimfanya ayaage mapema na kuwaacha wachezaji ambao majina yao sio makubwa kwenye masikio ya watu wakiendelea na michuano hiyo. Nyota huyo aliingia kama timu na kaka yake Jamie Murray, huku wakiwakilisha England, lakini umoja wao haukuwa na nguvu yoyote na kujikuta wakitolewa mapema katika raundi ya kwanza dhidi ya wapinzani wao kutoka nchini Brazil, Thomaz Bellucci na Andre Sa. Michuano ya Olimpiki iliwataka washinde kila mchezo ili waweze kusonga mbele kwenye hatua inayofuata, lakini ukipoteza mchezo inakuwa basi unayaaga mashindano na ndicho kilichotokea kwa nyota huyo na kaka yake ambapo walishindwa kutamba mbele ya bingwa wa mchezo huo ambaye anashika nafasi ya 55 kwa ubora duniani, Bellucci na Andre Sa, ambaye anashika nafasi ya 60 kwa ubora duniani.
4
Na MASYNENE DAMIAN -MWANZA KINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga, imevuna pointi tatu nyingine dhidi ya Alliance FC, katika mchezo uliochezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. Bao pekee la ushindi la Yanga lilifungwa na Amisi Tambwe dakika ya 75. Ushindi huo unaifanya Yanga kujizatiti kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo, baada ya kufikisha pointi 64, kupitia michezo 26, ikishinda 20, sare nne na kuchapwa mara mbili. Mchezo huo ulikuwa na vibweka kadhaa nje ya uwanja, ikiwemo mashabiki wengi kushindwa kuushuhudia kutokana na kukosa tiketi, sababu kuu ikiwa ni mfumo wa kielektroniki uliotumika katika kuchapa. Ilibainika kuwa mfumo huo wa kielektroniki uliwezesha kuchapwa tiketi 11,000 pekee, wakati uwanja huo una uwezo wa kuingiza watazamaji 30,000. Hatua hiyo iliwafanya viongozi wa Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA), kulazimika kutafuta tiketi za vishina ili kumaliza kadhia hiyo. Dakika ya tano tu ya mchezo, mwamuzi Shomari Lawi, aliizawadia Yanga penalti, baada ya mshambuliaji, Heritier Makambo, kuangushwa eneo la hatari na nahodha wa Alliance, Siraji Juma. Hata hivyo, Makambo alishindwa kuiandikia Yanga bao la kuongoza baada ya mkwaju wake wa penalti kupanguliwa na kipa wa Alliance, John Mwanda, kabla ya kuwa kona ambayo haikuzaa matunda. Dakika ya 21, Mkwaju wa Mapinduzi Balama, aliyepokea pande la kichwa la Bigirimana Blase, ulitoka nje ya lango la Yanga. Dakika ya 25, Dickson Ambundo wa Alliance, aliipangua ngome ya Yanga, lakini mkwaju mkali ulipanguliwa na kipa, Klaus Kindoki na kuzaa kona ambayo hata hivyo haikuzaa matunda. Dakika ya 29, Blaise alipoteza nafasi ya kuiandikia timu yake bao, baada ya kushindwa kuunganisha vema mpira wa kona uliochongwa na Ambundo. Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilikamilika kwa timu hizo kwenda mapumziko nyavu za kila moja ikiwa salama. Kwa ujumla kipindi cha kwanza, timu hizo zilishambuliana kwa zamu, lakini  umakini mdogo wa safu ya ushambuliaji ya kila upande ulisababisha kukosekana kwa mabao. Dakika ya 49, Kindoki, alifanya kazi nzuri baada ya kupangua kiki ya Ambundo kabla ya mpira kumfikia Blaise ambaye naye alipaisha. Dakika ya 58, Kocha wa Alliance, Malale Hamsini, alifanya mabadiliko, alimtoa Hussein Javu na kumwingiza Michael Chinedu, kabla ya kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera, kumtoa Mrisho Ngassa na nafasi yake kuchukuliwa na Mohamed Issa na Haruna Moshi ambaye nafasi yake ilizibwa na Amisi Tambwe. Dakika ya 63, Blaise alilimwa kadi ya njano baada ya kupinga maamuzi ya mwamuzi ambaye alikataa bao alilofunga kwa madai kwamba alikuwa ameotea. Dakika ya 75, Tambwe aliiandikia Yanga bao la kuongoza kwa shuti kali, baada ya kutengewa mpira na Makambo. Katika kutafuta namna ya kuchomoa  bao, dakika ya 81, Alliance ilifanya mabadiliko, alitoka Sameer Vicent na kuingia Richard John, kabla ya Yanga kufanya mabadiliko, ambapo alitoka Deus Kaseke na kuingia Said Juma. Dakika ya 86, Mohamed Issa, alilimwa kadi ya njano, baada ya kumchezea rafu Juma Nyangi wa Alliance. Alliance ilizidisha mashambulizi wakati huo kwa lengo la kutaka kuchomoa, lakini washambuliaji wake, Blaise, Ambundo na Chenedu, walikosa maarifa ya kuukwamisha mpira kimiani. Dakika ya 90, beki wa Alliance, Wema Sadoki, alilimwa kadi ya njano, baada ya kumsukuma, Feisal Salumu.  Hadi kipenga cha mwamuzi Lawi kinasikika kuashiria kumalizika kwa pambano hilo, Yanga ilitoka kifua mbele  kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji. Katika michezo mingine, Ruvu Shooting iliutumia vizuri uwanja wa nyumbani baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 6-2 dhidi ya Mwadui FC, Uwanja wa Mabatini, Pwani. JKT Tanzania ilitakata nyumbani Uwanja wa Meja Jenerali Michael Isamuhyo, Dar es Salaam, baada ya kuitungua Coastal Union bao 1-0, wakati KMC ililazimishwa suluhu na wageni wao Biashara United Uwanja wa Uhuru.
4
CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kina upungufu wa watumishi 1,200 kwani waliopo sasa ni 1,400 wakati wanaotakiwa kuwapo ni 2,600 ili kutosheleza mahitaji ya chuo.Akizungumza katika Mahafali ya Tisa ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), chuoni hapo, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Peter Msoffe alisema upungufu huo unachangia chuo hicho kushindwa kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi.“Chuo ili kutoa huduma kwa wanafunzi zaidi ya 40,000 kinatakiwa kuwa na watumishi 2,600 lakini kumekuwa na watumishi wachache katika kusaidia kutoa taaluma kwa ajili ya wanafunzi hao wengi na hivyo ingekuwa vema serikali ikasaidia kupata watumishi hao,” alisema.Mwenyekiti wa baraza la chuo hicho, Gaudentia Kabaka aliwataka wahitimu wa chuo hicho, kutoridhika na uhitimu huo, badala yake wajiongezee elimu ya ufundi na ujuzi mpya katika fani mbalimbali ili kuongezea fursa za ajira na kupanua uwigo wa ujasiriamali.Akizungumza wakati wa Mahafali ya Tisa ya chuo hicho, jjini hapa jana, Kabaka alisema pale inapowezekana, wasisite kujiongezea elimu ya ufundi na ujuzi mpya katika fani mbalimbali, hilo litawaongezea fursa za ajira na kupanua wigo wa ujasiriamali.“Uhitimu wenu, hata ule wa Shahada ya juu kabisa, ya Uzamili au Udaktari wa Falsafa (PhD), bado ni ufunguo tu kuwawezesheni kuyaona na kuyatafakari mazingira ya dunia mpya katika miono tofauti na makini inayolenga kubuni na kujenga misingi bora ya maisha na mahusiano ya binadamu,” alisema.
3
SERIKALI imedhamiria kuimarisha utabiri wa hali ya hewa nchini kufi kia uhakika wa utabiri kwa asilimia 95 baada ya kusaini mkataba wa ununuzi wa rada mbili za teknolojia ya kisasa, ambayo Tanzania inakuwa ya kwanza kuwa nazo katika Ukanda wa Afrika Mashariki.Rada hizo aina ya S-Band Radar zinazotengenezwa Marekani, zina teknolojia ya kisasa ambayo ni tofauti na zilizopo sasa za aina hiyo. Zitafungwa katika mikoa ya Mbeya na Kigoma. Mkataba wa ununuzi wa rada hizo, umesainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk Agness Kijazi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Ifratech Limites inayosimamia kazi za Kampuni ya Enterprise Electronics Corporation (EEC) ya Marekani, Edwin Kasanga.Makubaliano hayo yalishuhudiwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye, aliyesema ununuzi wa radi hizo umegharimu dola za Marekani 2,497,125 (sawa na Sh bilioni 5.7 kwa kila moja). Alisema serikali imejizatiti kuleta mabadiliko katika sekta hiyo nchini kwa maendeleo ya nchi, kwa kuhakikisha katika kipindi cha miaka mitano ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano, watahakikisha wanafunga rada saba zinazotakiwa ili utabiri wa hali ya hewa nchini uwe wa uhakika kwa asilimia 99.Alisema kwa sasa kuna rada mbili jijini Dar es Salaam na Mwanza, zinazowezesha utabiri kuwa wa uhakika kwa asilimia 88, lakini itakapokamilika ya tatu itakayokabidhiwa na kuanza kazi mkoani Mtwara Agosti mwaka huu na hizo mbili zitakazokabidhiwa baada ya miezi 14, utabiri utakuwa wa uhakika kwa asilimia 95. “Lakini baadaye ndani ya miaka hii mitano tutakapofunga nyingine mbili na kufikia saba zinazotakiwa utabiri utakuwa wa uhakika kwa asilimia 99,” alisema.Naibu Waziri alisema mkataba huo wa zaidi ya Sh bilioni 11 kwa zote mbili, ni kwa ajili ya kutengeneza, kuileta nchini, kufunga mpaka wanakabidhi serikalini. Aliitaka TMA kuhakikisha baada ya kuletwa na kufungwa rada hizo, kuvilinda vifaa na kutumia vizuri, kwani Watanzania sasa wanafuatilia kwa karibu huduma za hali ya hewa kutoka na kuwepo na wataalamu wa kutosha, wanaozalishwa katika chuo cha TMA Kigoma kinachonufaiha nchi nyingine za EAC.Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa TMA, Kijazi alisema kwa sasa wamesaini mkataba huo, lakini baada ya hatua za malipo na kila kituo zitatengenezwa na mpaka kufika nchini itachukua miezi 14 .Alisema kwa rada ya Mtwara, ambayo pia inatengenezwa na kampuni hiyo ya Marekani, ambapo mkataba wake ulisainiwa Oktoba mwaka jana itawasili nchini Agosti na kufungwa rasmi mkoani humo. Alisema rada hizo zitafungwa eneo la Kawetere mkoani Mbeya na Nayamoli, Kigoma huku zikiwa na uwezo wa kuona hadi kilometa za mkato 450 huku zikizunguka na uwezo halisi wa kuona mpaka matone madogo sana ya mvua ni kilometa za mkato 250.
3
UPANDE wa utetezi katika kesi ya utekaji mfanyabiashara maarufu, Mohammed Dewji maarufu ‘Mo’, inayomkabili dereva teksi, Mousa Twaleb, umeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuendelea kusikiliza kesi hiyo kwa sababu mteja wao amekaa muda mrefu mahabusu.Twaleb anakabiliwa na mashitaka ya utekaji wa mfanyabiashara huyo pamoja na utakatishaji fedha. Wakili wa utetezi, Mafulu Mbagwa, alitoa ombi hilo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, baada ya Wakili wa Serikali, Glory Mwenda, kueleza upelelezi bado haujakamilika.Wakili Mbagwa alisema mshitakiwa huyo amekaa mahabusu muda mrefu na kwamba washitakiwa wengine wanaokabiliwa na mashitaka hayo wako nje ya nchi. Alisema kama uwezekano wa kuwakamata washitakiwa wengine haupo, basi kesi hiyo iendelee na mshtakiwa huyo kwa kuwa walishaomba nakala ya hati ya kuwakamata washitakiwa wengine lakini hawajapewa.Hata hivyo, Hakimu Shahidi aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 23,mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na mshitakiwa amerudishwa rumande. Mahakama hiyo imeshatoa hati ya kuwakamata washitakiwa watano ambao ni Henrique Simbine, Daniel Manchice, Issac Tomo na Zacarious Junior ambao wote ni raia wa Msumbiji na Phila Tshabalala raia wa Afrika Kusini.Katika kesi hiyo, inadaiwa Mei Mosi na Oktoba 10, mwaka jana katika maeneo ya jiji la Dar es Salaam na Johannesburg, Afrika Kusini, kwa makusudi washitakiwa kwa pamoja waliendesha genge la uhalifu.Pia inadaiwa Oktoba 11, mwaka jana maeneo hoteli ya Colloseum wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, Twaleb pamoja na watu wengine ambao hawapo mahakamani, walimteka nyara MO na kumuweka maeneo ambayo ni hatari.Pia inadaiwa Julai 10, mwaka jana maeneo ya Mbezi Beach, wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, Twaleb alitakatisha fedha Sh milioni nane wakati akijua fedha hizo ni kosa la kushiriki genge la uhalifu na makosa ya kupanga.MO alitekwa Oktoba 11, mwaka jana majira ya alfajiri maeneo ya hoteli ya Colloseum wakati akienda kufanya mazoezi na alipatikana Oktoba 20, mwaka huo huo katika eneo la Gymkhana.
3
SERIKALI imesema inaandaa mpango wa hospitali, kutumia mapato ya ndani kuajiri watumishi wa afya.Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Usafi wa Mazingira na mkutano wa maofisa afya wa mikoa, halmashauri na wadau, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu Ummy alisema wanaandaa mpango ili hospitali zitumie mapato yake ya ndani kuajiri watumishi wa afya.Akizungumzia kuhusu changamoto ya tishio la ebola, alisema wataongeza maofisa kwa kuajiri watumishi 40 watakaofanya kazi mipakani.Pia alitaka kuwe na uwiano wa huduma za kinga na tiba, na kubainisha kuwa vifo vimepungua sana kutokana na kuwekeza kwenye chanjo na kufanikiwa kutokomeza magonjwa ya ndui pepopunda na kifaduro.Alisema ni lazima kuwekeza kwenye chanjo na suala la lishe kwa kuhakikisha huduma bora za lishe zinawafikia Watanzania.Aidha, alisema kila mwaka kiasi cha Sh bilioni 450 zinapotea kutokana na madhara ya uchafu na fedha hizo zingeweza kutumika kwa shughuli nyingine.Mkurugenzi wa Afya kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Dk Ntuli Kapologwe alisema wizara hiyo itashirikiana na Wizara ya Afya, kuandaa kikosi kazi kitakachobainisha changamoto zote za maofisa afya ili kuona namna ya kutatua changamoto hizo.
3
Na Gurian Adolf-Sumbawanga WACHIMBAJI wadogo wawili wamefariki dunia ndani ya mgodi, baada ya kukosa hewa safi walipokuwa kwenye shimo lenye urefu wa Mmita 21.5 na kuamua kuwasha mashine maalumu ya kutoa maji ndani ya mgodi huo ili waweze kuendelea na kazi ya kutafuta madini. Tukio hilo lilitokea Julai 23, saa 9:30 alasiri, katika Kijiji cha Kalundi, Kata ya Kipande, Tarafa ya Kate Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa. Waliofariki ni Justine Salawa (27) mkazi wa Kijiji cha Kalundi na Fredy Agustino Mkazi wa Kijiji cha Kaoze wilayani Sumbawanga. Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ralph Meela alisema wachimbaji hao waliingia kwenye shimo hilo wakiwa watatu na ghafla maji yalIibuka hali iliyosababisha kushindwa kuendelea na kazi hiyo, hivyo wakaamua kuwasha mashine ili kutoa maji hayo. Alisema baada ya kuwasha mashine hiyo, moshi ulitanda katika shimo hilo, hali iyosababisha kukosa hewa safi na kuzidiwa na hewa ukaa lakini mmoja wao alifanikiwa kutoka nje na kuokoa maisha yake, huku wengine wakishindwa kupata msaada wa haraka na kufariki dunia.  Meela alisema baada ya tukio hilo, jeshi la zimamoto na uokoaji lilifika katika eneo la tukio lakini kutokana na umbali walichelewa na walikuta watu hao wamefariki dunia na kufanikiwa kuitoa miili hiyo ndani ya mgodi huo kisha kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu na kukabidhiwa kwa ndugu kwaajili ya maziko. Alisema kuwa jeshi la polisi linamshikiria mmiliki wa mgodi huo kwa kosa la kuanzisha mgodi huo na kufanya uchimbaji wa madini bila kuwa na kibali. Alitoa wito kwa wananchi wanaomiliki migodi na maeneo ya machimbo ya madini kufuata taratibu na kuwa na vibali kwani Serikali itakuwa inawafanyia ukaguzi na kuwapa taratibu za kufanya shughuli zao bila kutokea kwa maafa yanayo epukika.
3
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza  hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi.  Kwa misingi kama hiyo sisi kama  chombo cha habari  tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk.  Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia.  Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”.  Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi,  Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii.  Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo.  Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge.  viongozi  wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo.
5
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustin Mahiga amekitaka Chuo cha Diplomasia nchini kutoa mafunzo mtambuka ili kukiwezesha chuo hicho kuzalisha wahitimu wanaoendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.Mahiga aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati wa mahafali ya 28 ya chuo hicho na kuongeza kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa kuwa pia itasaidia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya serikali iliyopo katika utekelezaji wa mpango wa uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo Mwaka 2025.Alisema ili kufikia malengo hayo, chuo hicho kinapaswa kufundisha diplomasi ya uchumi sambamba na uchumi wa viwanda ili kuzalisha wahitimu watakaoisaidia serikali kufikia malengo yake kwa kuwa chuo hicho kipo katika nafasi nzuri zaidi ya kufanya hivyo ikilinganishwa na vyuo vingine nchini.Balozi Mahiga alisema chuo hicho pekee katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kina mchango mkubwa katika kukuza masuala ya kidiplomasia, kwa sasa kinapaswa kuwa mstari wa mbele kuisaidia Serikali kwa kufundisha masomo yatakayoendana na mabadiliko hayo ya kiuchumi.“Naombeni maprofesa, walimu na wakufunzi watafsiri hilo na kuja na mipango itakayosaidia kuzalisha wahitimu watakaokuwa na uwezo wa kupata mitaji lakini wawezekezaji watakaokuja nchini kuwekeza katika maeneo mbalimbali kwa kuwa mambo haya yote yanahitaji diplomasia,” alisema Balozi Mahiga.Aliwataka wahitimu pia kutumia elimu waliyoipata kuwatafuta na kuwashawishi wawekezaji wa mataifa mengine, lakini pia kutambua heshima iliyonayo Taifa katika utatuzi wa migogoro mbalimbali na kuitumia nafasi hiyo kuilinda na kuiendeleza.Kwa upande wake, Mkuu Chuo cha Diplomasia, Dk Bernard Achiula alisema katika kuhakikisha chuo hicho kinaenda sanjari na mipango ya serikali kinatarajia, katika mwaka ujao wa masomo kitaongeza udahili wa wanafunzi hatua ambayo pamoja na mambo mengine kitasaidia kuzalisha wahitimu wa kutosha katika soko.Alisema hatua hiyo inatokana na mipango ya serikali ya kukiboresha chuo hicho baada ya kukipatia fedha za ujenzi wa majengo mbalimbali kiasi cha Sh bilioni mbili, jambo litakalosaidia kuongeza nafasi ya udahili kwa wanafunzi chuoni hapo.Aidha alisema katika kutimiza majukumu yake ya utoaji elimu, chuo hicho kimekuwa kikitoa mafunzo mbalimbali yakiwemo ya ushauri wa kitaalam, pamoja na elimu ya mahusiano, hatua iliyokifanya kizidi kujizolea sifa mbalimbali ndani na nje ya taifa.Naye Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Balozi Ombeni Sefue, pamoja na kuipongeza serikali kwa juhudi mbalimbali inazozifanya kukiboresha chuo hicho, alisema matarajio ya mbeleni kwa chuo hicho ni kuzalisha wahitimu watakaoleta tija kwa taifa.Alisema katika kufikia malengo ya serikali ya kuzalisha wataalam hao, chuo hicho kimeendelea kujikita katika mipango mikakati mbalimbali yenye lengo la kuendana na kasi ya mabadiliko ya serikali ya awamu ya tano ili kuliletea maendeleo taifa.
3
NAIROBI, KENYA MAKAMU Mwenyekiti wa Chama tawala cha Jubilee, David Murathe amesema Naibu Rais William Ruto anatakiwa kustaafu siasa pamoja na Rais Uhuru Kenyatta mwaka 2022. Mshirika huyo wa karibu wa Kenyatta amesema jamii yao ya Kikuyu haina Hati ya Makubaliano (MoU) na yeyote kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2022. Murathe alitoa kauli hiyo juzi huko Vihiga wakati wa sherehe za kimila za jamii ya Luhya zilizofanyika katika viwanja vya manispaa, Mbale. Kauli hiyo inaweza kumkasirisha Ruto, ambaye ana matumaini ya kuungwa mkono na Kenyatta atakapostaafu urais mwaka 2022. Murathe alisema Kenyatta na Ruto wanaongoza serikali kwa mihula miwili na wanapaswa kwa pamoja kustaafu baada ya kutumikia urais na unaibu rais. Viongozi akiwamo wa chama cha ANC Musalia Mudavadi Waziri wa Ugatuzi Eugene Wamalwa na kiongzi wa wafanyakazi Francis Atwoli na mamia ya wakazi walisherehekea tukio hilo la kila mwaka ambalo kwa kawaida hufanyika Desemba 26. “Iwapo William Ruto ana MoU na Uhuru Kenyatta, basi ni makubaliano baina ya watu wawili,” alisema Murathe. Aliongeza: “Iwapo wewe (Ruto) umeongoza na Uhuru kwa mihula miwili, nini tena unataka. Hatumjui mtu atakayetulinda bali tunamjua mtu atakayetusambaratisha. Tutamchukua mtu atakayehakikisha usalama wa Mlima Kenya.” Mwanasiasa huyo wa Jubilee, ambaye alishiriki shughuli hiyo ya umma hapo Vihiga kwa mara ya kwanza katika kile kinachoonekaa utayari kufanya ushirika na jamii ya Luhya, alisema chama chao kwa sasa hakina mgombea urais. Aliendelea kusema hakuna deni lolote kwani Uhuru na Ruto wameongoza serikali kwa usawa. Alisema ibara 148 (8) ya Katiba inakataza mtu kutumikia unaibu rais kama ilivyo kwa urais kwa mihula miwili. Hata hivyo, katiba haimzuii Naibu Rais kuwania urais. Murathe ameonekana kumvalia njuga Ruto kwa kupinga kura ya maoni hata kabla ya chama chao kutoa msimamo
2
.Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii nchini (TTB), imempa Muingereza Nick Reynald maarufu kama Bongozozo ubalozi wa utalii wa Tanzania nchini Uingereza.Akizungumza katika hafla ya kumkabidhi barua ya utambuzi kwa ajili ya kazi, Meneja Masoko wa TTB, Geofrey Meena amesema kuwa, Nick Reynald aliyezaliwa Zimbabwe na kuishi Tanzania kwa miaka 18 atakuwa balozi mzuri kwa utalii wa Tanzania kwa sababu anajua maeneo mengi ya utalii.“Nick Reynald ‘Bongozozo’ ameishi hapa nchini kwa miaka mingi kuanzia mwaka 1998, hivyo anauelewa utalii wa Tanzania, amekuwa maarufu sana hapa nchini kutokana na mapenzi makubwa kwa Tanzania ambayo yemejidhihirisha katika nyanja nyingi ikiwemo ushabiki wa mpira kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) pamoja na wachezaji akiwemo Mbwana Samatta anayekipiga kunako klabu ya mpira ya Aston Villa ya Uingireza,” amesema Geofrey Meena.TTB imedhamiria kukuza utalii kwa kuongeza watalii kutoka Uingereza kwa kuwa nchi hiyo ni ya pili kwa kuleta watalii wengi nchini ikitanguliwa na Marekani. Takwimu za utalii mwaka 2018 zinaonesha kuwa watalii kutoka Uingereza walikuwa 77,199 huku Marekani ikileta watalii 94,876.Kwa upande wake Bongozozo amesema kuwa yeye atakuwa balozi mzuri katika kutangaza mazuri ya Tanzania na utalii wake duniani kote kupitia mitandao yake ya kijamii ili kuleta watalii nchini.“Nikizunguka duniani kote kupitia mitandao yangu ya kijamii nitawaambia kuwa Tanzania ni nchi yenye watu wakarimu sana, nitazidi kuipeperusha bendera ya Tanzania na nitawaeleza sehemu za kitalii zilizoko Tanzania, kwa hiyo nimekubali kuitangaza Tanzania kwa watalii wengi duniani,” amesema Bongozozo.
3
Kauli hiyo ilitolewa juzi mjini hapa na Ofisa Mipango wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Dk Miraji Ukuti Ussi wakati akizungumza na waandishi wa habari wanaotembelea miradi mbalimbali ya maendeleo mjini Zanzibar.Alisema Dira ya Taifa 2020 na Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Zanzibar (Mkuza) kwa pamoja vinalenga kufikia ukuaji wa uchumi utakaowajali wananchi na zaidi masikini. Pia alisema mkakati huo umeainisha kwamba sekta za utalii na biashara ndizo mihimili mikuu katika ukuzaji huo.“Hivyo ni wazi kwamba utalii una jukumu kubwa katika ukuzaji uchumi wa Zanzibar na kupunguza umasikini,” alisema na kuongeza kuwa ndiyo sababu sekta hiyo inachangia GDP kwa asilimia 27 na fedha za kigeni asilimia 80.Alisema tokea kuanzishwa sera za kukaribisha vitega uchumi na sekta binafsi, asilimia 80 ya miradi iliyotekelezwa ni ile ya sekta ya hoteli na huduma za utalii ikiwa katika viwango mbalimbali.“Jumla ya hoteli 454 na nyumba za kulaza wageni zenye vyumba 7,421 viliweza kuhudumia kiasi cha wageni 169,223 kwa mwaka 2012.“Aidha Sekta ya Utalii imetoa mchango wa ajira ya moja kwa moja kwa vijana 13,017 na zaidi ya ajira 45,000 kwa zile nafasi zisizo na uhusiano wa moja kwa moja. Matarajio ni kuwa zaidi ya asilimia 50 ya waajiriwa wa Zanzibar watatokana na sekta ya utalii ifikapo mwaka 2020,” alisema.Pia alisema kampuni za kuongoza watalii zimeongezeka na kufikia 214 na kwamba huduma za usafiri wa ndani nazo zimeimarika na zile za usafiri wa anga na majini nazo zimeongezeka.Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wawekezaji Sekta ya Utalii Zanzibar (ZATI), Abdulsamad Said Ahmed, alisema sekta hiyo hivi sasa imepanuka na kumekuwa na mafanikio makubwa zaidi ukilinganisha na miaka iliyopita, kauli ambayo pia ilizungumzwa na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Waongoza Watalii Zanzibar (ZATO) Hassan Ali Mzee.Kwa upande wake Meneja Mauzo na Masoko wa Hoteli ya Hideaway upande wa Afrika Mashariki, George Kiruku alipongeza kuimarika kwa Sekta ya Utalii na kwamba kumesababisha kuwepo kwa hoteli za kuvutia hivyo kuzidi kuwapa hamu watalii kutembelea Zanzibar.
5
MWANDISHI WETU – DAR ES SALAAM MSOMI na mfanyabiashara maarufu Dar es Salaam, Tumaini Madinda, ameishauri Serikali kubuni njia mbadala itakayosaidia kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira kwa wasomi wengi wanaomaliza masomo yao hapa nchini. Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita alipozungumza na gazeti hili kwa nia ya kuisaidia Serikali kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ambalo zaidi linawakumba vijana na kuongezeka kila kukicha.  Madinda aliyezaliwa mkoani Dodoma miaka arobaini iliyopita, alifafanua kuwa zinahitajika juhudi za makusudi kwa Serikali, hasa wizara ya elimu kuhakikisha inaweka mikakati ya kimitaala ili kuzalisha wahitimu wanaoweza kujiajiri. “Mimi nimehitimu shahada ya juu (Masters) ya masuala ya uwekezaji na fedha pale Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), nikaajiriwa sehemu mbili tatu kabla ya kutafakari njia mbadala iliyoniwezesha kujiajiri,” alisema Madinda. Aidha, alisema kutokana na uongozi madhubuti wa Rais John Magufuli, anaamini Wizara ya Elimu inaweza kuwatumia wataalamu wa ndani na hata wa nje kuanzisha mfumo huo anaouona kama mwarobaini wa tatizo hilo. “Ombi langu kwa Serikali kupitia wizara yenye dhamana ya elimu ni kwamba, wabuni njia mwafaka ziatakazozaa matunda kwa vijana na hasa watoto wetu ambao watakapofikia ngazi ya elimu ya juu watoke na ujuzi na maarifa yatakayowasaidia kujiajiri,” alisema Madinda. Aliongeza kuwa: “Nikipata nafasi ya kuzungumza na vijana waliohitimu vyuoni na wanaoendelea na masomo, nitawashauri kukazania maarifa huku wakizingatia kuwa ajira zao zitatokana na wao wenyewe, kinyume na wengi wanaotegemea Serikali au taasisi binafsi kuwaajiri.” Akizungumzia maisha yake kwa sasa, Madinda alisema anajishughulisha na biashara mbalimbali huku akimiliki kampuni za ulinzi na forodha akiwa ameajiri Watanzania wengi. Kama haitoshi, anamiliki mashamba makubwa mikoa ya Pwani na Dodoma na utoaji wa ushauri.  “Kama vijana wa Tanzania tutaendelea kuiendekeza kasumba ya ‘utegemezi’ wa kuajiriwa, tutazidi kuchelewa. Lazima tuamke sasa, dunia inakwenda kasi sana, hatuna budi kuchangamka. Sayansi na teknolojia imetamalaki kila mahali, tuongeze juhudi na kutumia maarifa kuyafumbata maendeleo,” alisema Madinda.
3
NA MWANDISHI WETU WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Dk. Frida Mokiti  kubadilisha uongozi wa  Kituo cha Afya cha Levolosi baada ya kulalamikiwa kutoa huduma mbovu kwa wajawazito. Pia amewataka wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kujenga hospitali za wilaya ili kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali za rufaa. Majaliwa alitoa agizo hilo jana alipotembelea  Hospitali ya Mkoa ya Mount  Meru, ambapo alisema tatizo la msongamano wa wagonjwa hospitali za rufaa na hospitali nyingine ni lazima lipatiwe ufunguzi. “Hatuhitaji kuwa na madaktari ambao wanasumbua wagonjwa. Daktari wa Mkoa hakikisha kile kinacholalamikiwa kule Levolosi kinatafutiwa ufumbuzi. “Hapa Mount Meru hakikisheni mnaboresha mazingira ya vyoo kwenye wadi  za wazazi pamoja na kujenga sehemu ya kuoshea vyombo kwa wagonjwa, ” alisema. Awali alipotembelea wodi ya kinamama wanaosubiri kujifungua, mmoja wa wagonjwa, Glory Paul Mkazi wa Olasiti alimweleza Waziri Mkuu kuwa mtoto wake alifia tumboni baada ya wauguzi na  madaktari wa kituo cha Afya cha Levolosi  kuchelewa kumpatia matibabu. “Wakati nahudhuria kliniki nilishaambiwa na daktari kuwa natakiwa kujifungua kwa njia ya upasuaji na siwezi kujifungua kwa njia ya kawaida, nilimwambia nesi kuwa  natakiwa kufanyiwa upasuaji wakanikatalia na kunilazimisha nijifungue kwa njia ya kawaida ambapo ilishindikana na baada ya muda waliniambia kuwa mtoto amekufa na wananifanyia upasuaji ili kuokoa maisha yangu,” alisema. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia alisema amepokea maagizo ya Waziri Mkuu, ambayo yanalenga kuboresha utoaji wa huduma bora kwa wananchi na kusisitiza kuwa awali alichukua hatua za kinidhamu kwa watoa huduma za afya kituoni hapo na ataendelea kusimamia nidhamu ya kazi ili kuondoa malalamiko kwa wananchi juu ya huduma za afya.
3
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo imezindua huduma mpya itakayowezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati nchini kuwa pamoja kibiashara.Huduma hiyo ya ‘Office internet’ ilizinduliwa jana jijini Dar es Salaam kupitia kitengo cha biashara cha kampuni. Ofisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, Pavan Ramadhani aliwaambia waandishi wa habari kuwa huduma ina mfumo wa kisasa uliounganishwa na programu za Microsoft Excel, Power Point na Outloot. Alisema mfumo una uwezo wa kuunganisha zaidi ya wafanyabiashara 32 ambao wataweza kubadilishana mawazo kwa pamoja, kufanya mkutano wa pamoja kwa njia ya video kwenye simu, kuhariri kazi moja kwa pamoja na kupangiana mikakati ya kazi.Alisema ili mtu aweze kupata huduma hiyo, lazima aingie mkataba na kampuni kwa muda usiopungua miaka miwili kabla ya kukabidhiwa kifaa kitakachoweza kuunganishwa apate huduma husika.“Tulifanya kazi kwa ushirikiano wa karibu sana na wateja wetu, ambao walituonesha maeneo matatu muhimu yenye changamoto, kwanza kuunganisha huduma ya intaneti ya kasi, ukosefu wa maana halisi ya matumizi ya intaneti na mwisho uhusiano na biashara,” alisema.
3
UKOSEFU wa umeme wa uhakika umetajwa kuwa changamoto kubwa inayokwamisha uzalishaji kwenye mgodi wa dhahabu wenye leseni namba PML 0000829SWZ uliopo wilayani Chunya mkoani Mbeya.Hayo yalibainishwa na Meneja wa Mgodi huo, Shigongo Kimogele kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila aliyezuru akilenga kujua uzalishaji unaofanyika mgodini hapo.Kimogele alisema kwa muda mrefu sasa wamekuwa na changamoto ya umeme wa uhakika, hali inayosababisha shughuli za uzalishaji na nyinginezo kutokuwa za uhakika.Meneja huyo alitaja changamoto nyingine kuwa ni kukosekana kwa mawasiliano ya uhakika ya simu.“Changamoto nyingine ni kutoeleweka vizuri kwa jiolojia ya eneo hili na uwepo wa maji mengi katika ardhi ya eneo hili. Hii inafanya gharama za uchimbaji kuwa za juu sana.“Pia uwepo wa leseni kubwa za utafiti wa madini katika eneo la Itumbi unafanya uwezekano wa kupanua shughuli zetu za uchimbaji mdogo wa nje ya eneo la leseni hii kuwa mdogo.“Pamoja na changamoto hizo tunaishukuru serikali kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa msaada na ushirikiano mkubwa ambao tumekuwa tukiupata, pia Wizara ya Madini kwa ushirikiano mkubwa katika kazi zetu za uchimbaji.Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila aliahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa makampuni yote yanayojishughulisha na shughuli za uchimbaji madini mkoani hapa hususani katika kutafuta suluhu ya changamoto zinazowakabili wachimbaji ili kuleta ufanisi kwenye utendaji kazi wao.Alisema serikali imejipanga kuhakikisha inawaondolea vikwazo wachimbaji wa madini ili shughuli zao ziweze kuwa na tija na mchango kwenye Serikali ya Awamu ya Tano iliyolenga kuwaletea maendeleo Watanzania.
5
RIPOTI ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya kipindi cha miezi sita ya mwaka huu, 2018 inaonesha kuongezeka kwa kiasi kikubwa kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto hasa wa kingono aina ya ubakaji na ulawiti mara tatu zaidi ikilinganishwa na kipindi cha mwaka jana. Hayo yamebainishwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa kituo hicho, Anna Henga wakati wa uzinduzi wa ripoti ya nusu mwaka ya haki za binadamu kwa mwaka huu kuanzia Januari hadi Juni.Henga alisema mwaka jana, matukio yalikuwa 12 na mwaka huu 533 yaliyoripotiwa. Alisema kati ya matukio 6376 ya ukiukwaji wa haki za watoto, matukio 2,365 yametokana na ubakaji na 53 ni ulawiti. Pia alisema vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake hususani ukatili wa kingono na kimwili vimeongezeka na akatolea mfano wa vitendo vya ubakaji wa wanawake kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2018 ambapo wanawake zaidi ya 1,218 wameripotiwa kubakwa huku ikikadiriwa kuwa ni wanawake 203 kila mwezi.Alisema ripoti hiyo imeonesha kupungua kidogo kwa mauaji ya imani za kishirikina na kujichukulia sheria mkononi. “Mauaji ya imani za kishirikina yamepungua kutoka 172 hadi 106,” alisema Henga. Aidha, alisema ripoti imeonesha kuongezeka kwa hofu miongoni mwa watu wenye ulemavu wa ngozi wakati Tanzania ikielekea kwenye chaguzi mwaka 2019 na 2020.Alisema pia ripoti hiyo imeelezea changamoto katika mazingira ya elimu hasa upungufu wa vyoo ama matundu ya vyoo mashuleni. Alitolea mfano katika Shule ya Msingi ya Ichenjezya wilayani Mbozi mkoani Songwe ambapo iliripotiwa kwamba wanafunzi zaidi ya 1,300 wanatumia matundu manane ya choo peke yake.
3
Amelitaka baraza hilo lifanye tathmini kuhusu namna ya kuunganisha mifuko hiyo bila ya kuathiri majukumu ya msingi na mantiki ya kuanzishwa kwake. Alitoa agizo hilo juzi wakati akifungua maonesho ya mifuko ya uwezeshaji katika Uwanja wa Mashujaa mjini Dodoma.“Lengo ni kuwa na mifuko michache, lakini inayobadilisha maisha ya wanufaika, ambao ni wananchi. Nitafurahi kupata taarifa hiyo kabla au ifikapo Mei, 2018,” alisema. Akaongeza, “Uwezeshaji wananchi kiuchumi ni jambo ambalo lipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/2017- 2020/2021”.Alisema mifuko hiyo imesaidia upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali na kupunguza kiwango cha umaskini nchini. “Hadi kufikia mwaka 2016 Mifuko hiyo kwa pamoja ilikuwa imetoa mikopo yenye thamani ya sh trilioni 1.759 kwa wajasiriamali 400,000.Awali Katibu Mtendaji wa NEEC, Beng Issa alisema kati ya mifuko 19 ya uwezeshaji, mifuko 13 imeweza kushiriki katika maonesho hayo ya kwanza nchini. Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPB Bank PLC, Sabasaba Moshingi alisema kwa niaba ya washiriki wengine kuwa, maonesho hayo yalilenga kukuza uelewa wa watu kuhusu uwepo wa mifuko ya kuwezesha wananchi kiuchumi na fursa zitolewazo na mifuko hiyo.
5
Lazaro amerithi mikoba ya aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, John Tamba ambaye ni mwajiriwa wa Jeshi hilo aliyepumzishwa pamoja na baadhi ya viongozi wa benchi la ufundi kwa siku za hivi karibuni, kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo, mnamo Desemba 26, mwaka huu 2015.Katika mchezo wake wa kwanza tangu kukabidhiwa timu hiyo uliofanyika Desemba 26, mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri wa mjini hapa, Polisi Moro ilitoka sare ya kufungana bao 2-2 na wapinzani wao wa jadi timu ya soka ya Bukinafaso zote ya mjini Morogoro.Hivyo alisema, baada ya kuangalia mchezo wake wa kwanza dhidi ya timu ya Bukinafaso, jukumu kubwa linalomkabili ni namna ya kuijenga timu iwe na utulivu na umakini kwa wachezaji katika uchezaji wanapokuwa mchezoni kwa kuwa ni nyenzo ya kuiwezesha timu kupata ushindi.“Sare hii imenionesha mapungufu na imenipa mwanga wa timu nzima na hivyo kuwa na sehemu ya kuanzia maeneo ya kuyafanyia kazi kwa haraka ili kuwezesha kupata ushindi michezo ijayo,” alisema Lazaro.Lazaro ambaye aliipandisha Ligi Kuu timu ya Mgambo Shooting tangu alipoanza kuinoa ikiwa ligi daraja la tatu ngazi ya taifa mkoani Tanga, alisema kuwa uelewano wa wachezaji kitimu ndiyo msingi mkuu wa kuwa na timu imara zaidi kwa kila mchezo utakaokuwa mbele yao.Kocha mkuu huyo ambaye aliwahi kuichezea timu ya Yanga katika nafasi ya beki kati ya mwaka 1992 na 1993, alisema kinachohitajika kwa sasa ndani ya timu hiyo ni umoja kati ya viongozi, mashabiki na wachezaji.Baada ya matokeo hayo, Polisi Moro imefikisha pointi 11 , wakati vijana wa Bukinafaso wakiwa na pointi tatu hadi sasa katika kundi lao la B lenye timu nane. Timu nyingine kwenye kundi hilo ni Kurugenzi na Lipuli za Iringa, JKT Mlale ya Ruvuma, Ruvu Shooting ya Pwani, Njombe Mji ya mkoa wa Njombe na Kimondo ya mkoa wa Mbeya.
4
Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, amejiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari na kuhimiza wananchi kufanya hivyo, kwani moja ya faida kubwa ni kujihakikishia kuwa na bima ya afya. Akizungumza jana baada ya kutembelea banda la PSPF lililoko jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere maarufu Sabasaba wakati wa Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea. “Mimi nitoe wito kwa wananchi kujiunga zaidi na mpango huu kwani watafaidika na huduma ya afya na nyinyi muongeze kasi ya kutoa elimu kwa wananchi ili wajiunge zaidi,” alisema Dk. Mpango. Dk. Mpango pia alikabidhiwa kadi yake ya uanachama muda mfupi baada ya kujiunga. “Mheshimiwa, Mpango wa Uchangiaji wa Hiari una faida nyingi na tumewalenga hasa watu wa kawaida kama vile wajasiriamali, wakulima, mama lishe, bodaboda na machinga na tumekuwa tukipata watu wengi wanaokuja kujisajili na mpango huu na wengi wao wamevutiwa na hii Bima ya Afya ambayo ni moja ya faida azipatazo mwananchama,” alisema Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, wakati akimkabidhi kadi yake Waziri Mpango
3
JESHI la Polisi nchini limesema linafuatilia kwa karibu maoni, yanayotolewa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kifo cha Mmiliki wa Kampuni za IPP, Dk Reginald Mengi ili kujiridhisha kama kweli kifo chake, kimetokana na mkono wa mtu au ni kifo cha kawaida.Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro alipofika nyumbani kwa Mengi jijini Dar es Salaam jana kwa ajili ya kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki.IGP Sirro alisema Jeshi lake linafuatilia yote, yanayozungumzwa kwenye mitandao na kama itabainika kifo cha Dk Mengi, kimetokana na mkono wa mtu, sheria itachukua mkondo wake, kwa kuwa hakuna aliye juu ya sheria.Lakini, pia alisema wanafanya hivyo ili kujiridhisha wasije wakamuonea mtu yeyote kwa sababu ya mitandao.Aliwataka wananchi watulie, kwa kuwa yote yanayoelezwa mitandaoni wameyachukua kwa uzito wake. Alisema Jeshi hilo limefungua kadokezo kwa ajili ya kufuatilia hayo yote, yanayozungumzwa ili kuona kuna ukweli kiasi gani.“Jambo la msingi tumalize kwanza msiba, hayo yanayozungumzwa mitandaoni tunayafuatilia, tukiingiza mambo mengi wakati wa shida, tunaweza kupoteza mwelekeo, nilikuwa napitia na utaona kila mtu ana maoni yake, niwaombe tu wananchi watulie,”alisema IGP Sirro.Akimzungumzia Dk Mengi, IGP Sirro alisema alikuwa na tabia ya unyenyekevu, aliheshimu watu na alijishusha licha ya uwezo mkubwa aliokuwa nao, jambo ambalo ni nadara kuliona kwa matajiri wengi.Alisema taifa limempoteza mdau muhimu katika masuala ya ushauri.Kikwete Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, alisema kuwa taifa limepoteza mmoja wa raia wake makini, mchapakazi na mahiri.Lakini, alisema yeye binafsi amempoteza mtu ambaye kwake alikuwa kama rafiki, kaka na ndugu wa karibu.Kikwete alisema Dk Mengi ni mtu aliyeipenda nchi yake na maendeleo ya taifa lake, ameishi maisha yake na kufanya mambo mengi, lakini pia amekuwa mtu wa aina yake na alitumia utajiri wake kuwasaidia wengine walio na mahitaji mbalimbali.“Taarifa ya kifo chake kweli ilinistua kwa sababu ni jambo ambalo sikulitarajia, lakini kifo hakina taarifa. Tulizungumza kwa simu na kukubaliana kuwa yeye atakaporudi na mimi nitakaporudi kutoka safari, tungekutana kwa mazungumzo yetu ya kawaida, tumekuwa tukikutana kila mara na kuzungumza,”alieleza Kikwete.Aliwataka wanafamilia kuwa na moyo wa uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu walichonacho.Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji nchini (TBC), Dk Ayoub Rioba, amesema miongoni mwa mambo makubwa ambayo Dk Mengi aliyafanya enzi za uhai wake, si tu kubadilisha maisha yake binafsi, bali na maisha ya watu wengine.Alisema Dk Mengi pia ameliachia taifa urithi mkubwa wa kitabu chake kinachoitwa “I CAN, I MUST, I WILL”, lakini pia amesaidia kuhamasisha vijana nchini kuwa na fikra chanya wakati wote pamoja na kujiamini kwamba wanaweza kubadilisha maisha yao na kusaidia wengine.DC mstaafu Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Baraka Konisaga, alisema kuwa siyo rahisi kupata mtu wa aina ya Dk Mengi na inaweza kupita miaka mingi kupata mtu wa aina hiyo.Alisema namna bora ya kumuenzi Dk Mengi ni kuendelea kuutumia ushauri wake katika mambo mbalimbali ili kuyaendeleza yale mazuri aliyoyaamini na kuyapigania enzi za uhai wake.Dk Mengi alifariki Dubai katika Falme za Kiarabu (UAE), usiku wa kuamkia juzi Alhamisi, Mei 2 baada ya kuugua kwa muda mfupi.Kwa mujibu wa Mwanasheria wake ambaye pia ni Msemaji wa Familia, Michael Ngalo mwili wa Mengi utawasili kesho kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates saa 8:00 mchana.Alisema baada ya kupokelewa, utapelekwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo huku waombolezaji wakiendelea kuomboleza nyumbani kwa marehemu.Ngalo alisema Jumanne asubuhi mwili utapelekwa katika Viwanja vya Karimjee ili wananchi na viongozi mbalimbali, wakiwemo wafanyabiashara wenzake wapate nafasi ya kutoa heshima za mwisho kabla ya kupelekwa nyumbani kwake.Kwa mujibu wa Ngalo, Jumatano mwili utasafirishwa asubuhi kwenda Kilimanjaro kwa ndege na utapokelewa katika Uwanja cha Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kisha kupelekwa nyumbani kwake Machame katika kijiji cha Nkuu kwa maziko yatakayofanyika Alhamis asubuhi, Mei 9 yakitanguliwa na ibada itakayofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) la Kisereny.
3
WAKATI zikiwa zimebaki siku chache kabla ya mkutano wa wakuu wa serikali na nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kufanyika nchini, umma wa Watanzania umesisitizwa kujiandaa kuutumia kwa fursa ya maendeleo.Katika kufanikisha hilo, vyombo vya habari vimetakiwa kuwa mstari wa mbele kuhabarisha umma juu ya jumuiya kwa kuanisha fursa zikiwamo za kibiashara zitakazopatikana kutokana na mkutano huo ambao watu wapatao 1,000 wanatarajiwa kuwa nchini wakiongozana na wakuu wa nchi.Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Agnes Kayola aliwaambia waandishi wa habari hivi karibuni kwamba mkutano wa 39 SADC utatanguliwa na maonesho ya wiki ya viwanda yatakayofanyika Agosti 5 hadi 8.Utafuata mkutano wa makatibu wakuu na wataalamu utakaofuatiwa na mkutano wa mawaziri kabla ya ule wa wakuu wa nchi na serikali za nchi wanachama wa SADC utakaofanyika Agosti 17 na 18.Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza ni miongoni mwa viongozi waliosisitiza umuhimu wa kuelimisha umma juu ya fursa za kiuchumi na kijamii zitokanazo na mkutano huo utakaofanyika jijini Dar es Salaam.Akifungua mafunzo yaliyoandaliwa hivi karibuni kwa ajili ya waandishi wa habari watakaoripoti mkutano huo, Shonza alitaja baadhi ya fursa ambazo Watanzania hawana budi kuzifahamu ni pamoja na kwenye usafiri na usafirishaji,masoko, malazi, burudani na utalii.“Kila mwandishi wa habari analo jukunu la kutangaza fursa zilizopo katika jumuiya yetu ya SADC,” alisema na kutaja fursa hizo ni pamoja na kupata masoko ya bidhaa za viwandani na mazao ya kilimo yanayozalishwa katika nchi wanachama 16 zenye idadi ya watu wasiopungua milioni 450.Aidha, watoa mada katika mafunzo hayo ya kujengea waandishi uwezo kuandika na kuripoti habari za SADC yaliyofanyika hivi karibuni mjini Morogoro, walihimiza umma kufahamishwa fursa za za mkutano sambamba na uanachama wa Tanzania kwenye jumuiya.Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino, Dk Kaanaeli Kaale aliwataka waandishi kuandika na kuripoti habari za SADC sasa na kipindi chote Tanzania itakapokuwa mwenyekiti kujengea wananchi uwezo wa kuelewa na kutumia fursa zilizopo.Katibu Mkuu mstaafu Ofisi ya Waziri Mkuu, Mussa Uledi alisisitiza umuhimu wa jamii kufahamu umuhimu na malengo ya jumuiya. “Lengo la SADC ni kufungua masoko na kujenga uwezo kwa nchi wanachama kushindana katika masoko ya kimataifa,” anasema.Uledi alisema mchango wa SADC katika kuchochea maendeleo ya nchi wanachama ni mkubwa na wa kuenziwa.Alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwanzo Afrika zilizotoa na kuratibu mtangamano wa kikanda.Alisema mkakati wa maendeleo wa SADC unafanana kwa kiwango kikubwa na wa Tanzania unaozingatia haja ya uendelezaji viwanda na miundombinu.“Hivyo Tanzania haina budi kuendelea kutumia mtangamano wa kikanda kama nyenzo ya kibiashara ya kuendeleza mauzo ya bidhaa na huduma nje na pia kupunguza umasikini,” alisema.Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk Ayub Rioba (pichani) alisema, “Kuna habari nyingi zinazohusu mambo mazuri ya Afrika zinapaswa kuandikwa na kuripotiwa na vyombo vya habari… Waandishi wa habari wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa wanatangaza mambo mazuri ya Afrika.”Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Agnes Kayola alisema maonesho ya biashara yatatumika kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini na nchi wanachama wa SADC.Wengine waliosisitiza wananchi kutumia mkutano huo kuwa fursa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Balozi Herbert Mrango.Balozi Mrango alisema vyombo vya habari vinalo jukumu kubwa kujenga uelewa kwa wananchi wa nchi wanachama watumie fursa hizo. Kaulimbiu ya mkutano ni ‘Mazingira wezeshi ya biashara kwa ajili ya maendeleo jumuishi na endelevu ya viwanda’.Tanzania inakuwa mwenyeji wa mkutano huu ikiwa ni miaka 16 tangu ilipopata fursa hiyo mwaka 2003.Nchi wanachama wa SADC ni Tanzania, Namibia, Zimbabwe, Zambia, Malawi, Afrika Kusini, Botswana, Angola, Msumbiji, Eswatini, Lesotho, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mauritius, Comoro, Shelisheli na Madagascar.
3
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imesema imeshaanza uchunguzi na itawahoji wale wote waliohusika kwenye mkataba mbovu, uliosainiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na kuisababishia nchi hasara.Amesema ndani ya wiki tatu, kazi hiyo itakuwa imekamilika. Katika hatua nyingine, Takukuru imesema mbali na kuanza uchunguzi, pia wameshaanza kuwahoji baadhi ya wahusika wa mkataba huo. Imesisitiza kuwa itafanya hivyo, bila kujali wadhifa wa mtu yeyote, aliyehusika katika sakata hilo.Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo alipozungumza na Habarileo.Mbungo amesema wataifanya kazi hiyo bila kujali wadhifa wa mtu yeyote na kuwa uchunguzi wa jambo hilo, ulishaanza tangu siku ya kwanza Rais Dk John Magufuli alipowatengua viongozi hao wakati akizindua nyumba za askari Magereza.“Rais akishasema kinachofuata ni utekelezaji tu. Takukuru tulianza uchunguzi wa jambo hili tangu siku ya kwanza alipotamka wakati akifungua nyumba za askari Magereza. Tulipotoka tu pale Magereza tulikusanya nyaraka zote siku hiyo hiyo ukiwemo mkataba na nyaraka zingine, kwa hiyo kwa sasa tuko hatua 100 mbele kwenye kulichunguza jambo hili,”amesema Brigedia Jenerali Mbungo.Alisema kwa sasa hawezi kusema ni watu wangapi wameshawahoji, kwa kuwa kazi hiyo wanaifanya kwa siri ili kuzuia watu wasiifuatilie, lakini pia inahusisha nchi nyingine na watahitaji kupata taarifa kamili kutoka huko.Mbungo alifafanua kuwa kauli hiyo ya Rais, ilikuwa hamasa ya kuwataka wafanye uchunguzi kwa haraka bila woga, hata kama wizara hiyo inaangukia katika vyombo vya ulinzi na usalama.Wakati akizindua nyumba za Askari Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam Januari 23 mwaka huu, Rais Magufuli alisema hakuna wizara inayomtesa, kama Wizara ya Mambo ya Ndani kutokana na miradi ya hovyo iliyokuwa inafanyika.Rais Magufuli aliweka bayana kuwa wizara hiyo iliingia mkataba wa ajabu hivi karibuni wenye thamani ya Euro milioni 408, sawa na Sh trilioni 1.2 kwa ajili ya kununua vitu mbalimbali zikiwemo ‘drones’ , huku wahusika wakipewa dola 800 na kompyuta mpakato kila walipokutana kwa mazungumzo.Kutokana na mkataba huo, Rais aliamua kutengua uwaziri wa Kangi Lugola na kumwondoa katika nafasi yake Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye na kuitaka Takukuru kulichunguza suala hilo.Rais Magufuli alimtaja Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuwa ni miongoni mwa watu, waliohusika kwa asilimia 100 kuhusu mkataba huo mbovu na amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene kulifanyia kazi suala hilo, baada ya kumkabidhi nyaraka zote zinazohusika.
3
Asha Bani-Dar es Salaam Upatikanaji wa taarifa kamili kuhusu rushwa ya ngono bado ni tatizo kubwa kutokana na jambo hilo kuonekana kuwa la usiri katika jamii. Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano Novemba 26 na Mkurugenzi wa Mfuko wa Uhifadhi Wanawake Tanzania (WFT), Mary Rusimbi wakati wa kongamano la kujadili masuala ya Rushwa ya ngono ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia. Kongamano hilo limeandaliwa na Mfuko wa Wanawake nchini (WFT), Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) na mabalozi wa nchi za Ireland na Uholanzi likiwa na kaulimbiu ‘Kataa rushwa ya Ngono Jenga Kizazi chenye usawa’. Amesema ni vema mapambano juu ya rushwa ya ngono yanahitaji kuongozwa na utafiti ili kujua ni wapi wanaweza kuanzia katika kupambana na rushwa hiyo ambayo ni jambo la kikatili. “Hadi sasa kuna asilimia 98 ya unyanyasaji wa kijinsia hivyo ni muhimu jambo hili kushirikisha watu wote hususani ngazi za familia kutoa ushirikino na kuhakikisha watu wanaofanya vitendo hivyo kuchukuliwa hatua za kisheria,” amesema Mary. Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Jeshi la Polisi, Janeth Magomi amesema jeshi hilo ni wasimamizi wa sheria na wamekuwa wakifanya kazi katika shuleni, vyuoni na maofisini katika kuhakikisha wanatoa elimu juu ya rushwa ya ngono na ukatili wa kijinsia. Naye Mkurugenzi wa Tamwa, Rose Reuben amesema kulazimisha ngono na kutoa rushwa ya ngono kwa namna yeyote ni kosa la jinai. “Jamii ina jukumu kubwa la kutoa taarifa na kuhabarishana kwasababu rushwa ya ngono ina madhara makubwa ikiwamo maambukizi ya maradhi ya ugonjwa wa Ukimwi kuongezeka kwa kasi. “Maadili kwa sasa yamebadilika na teknolojia imeongezeka, hivyo ni vyema taarifa za rushwa ya ngono na unyanyasaji mwengine wa jinsia ufanyiwe kazi na upingwe kwa kuunganisha nguvu ya pamoja na wadau mbalimbali,” amesema Rose.
3
    KHARTOUM, SUDAN RAIS wa Sudan, Omar el-Bashir, amekataa mwaliko kutoka utawala wa Saudia Arabia wa kuhudhuria mkutano wa mataifa ya Kiislamu ambao Rais Donald Trump atakuwa mgeni rasmi. Bashir, ambaye alitoa sababu za kibinafsi, anasakwa kwa uhalifu wa kivita katika eneo la Darfur na Marekani ilikuwa haikufurahia mwaliko wake katika mkutano huo. Sudan ilikuwa imesema kuwa inataka kuimarisha uhusiano wake na Marekani katika mkutano huo. Saudia ndilo taifa la kwanza la ziara ya kigeni ya Trump. Taarifa ya Ofisi ya Rais Bashir ilisema kuwa rais huyo aliomba msamaha kwa Mfalme Salma wa Saudia kwa kushindwa kuhudhuria mkutano huo wa Riyadh. Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa juu ya uamuzi huo. Waziri wa masuala ya mataifa ya kigeni, Taha al-Hussein, atamwakilisha. Mwaka 2002 na 2010, mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita (ICC) ilitoa agizo la kukamatwa kwa Rais Bashir kwa mauaji ya halaiki, uhalifu wa kivita na uhaifu dhidi ya binadamu katika eneo la Darfur, ambapo takriban watu 300,000 waliuawa.
2
NA JUDITH PETER, DAR ES SALAAM MSHAMBULIAJI wa kimataifa kutoka Burundi, Didier Kavumbagu na beki mahiri Aggrey Morris wa Azam FC, wameanza rasmi mazoezi baada ya kupona majeraha yaliyokuwa yakiwakabili. Morris alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya goti tangu Novemba mwaka jana, alipoumia wakati akiwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Zanzibar, ‘Zanzibar Heroes’, iliyokuwa ikijiandaa na michuano ya Kombe la Chalenji iliyofanyika nchini Ethiopia. Mwezi uliopita mlinzi huyo alipelekwa jijini Cape Town, Afrika Kusini, katika Hospitali ya Afrisurb kufanyiwa matibabu ambapo alitakiwa kupumzika kwa takribani wiki tatu kabla ya kuanza mazoezi. Kwa upande wake Kavumbagu, alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya enka aliyopata wakati wa mchezo wa Kombe la Mapinduzi mwezi uliopita dhidi ya Yanga, uliofanyika visiwani Zanzibar. Kwa mujibu wa daktari wa timu hiyo, Juma Mwimbe, Morris ameanza na mazoezi ya gym ambayo atafanya kwa muda wa wiki moja, kabla ya kuhamia kwenye mazoezi mepesi ya uwanjani kwa muda wa wiki moja. “Morris ameanza mazoezi ya gym ili aweze kuwa fiti zaidi kutokana na kukosa mechi kwa muda mrefu, lakini baada ya hapo atajiunga na wenzake uwanjani mara baada ya timu kurejea kutoka Mbeya, ambako tutacheza na Mbeya City na Tanzania Prisons,” alisema. Mwimbe alisema Kavumbagu naye alianza mazoezi ya gym jana, ambayo atafanya kwa siku kadhaa kabla ya kuanza mazoezi na wenzake uwanjani. “Programu ya Kavumbagu kabla ya kurejea uwanjani ni fupi kwa kuwa hajakaa nje muda mrefu,” alisema Mwimbe. Kurejea dimbani kwa nyota hao, kutaleta manufaa kwa timu hiyo inayokabiliwa na michuano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho, ambapo Azam wamepangwa kuanzia raundi ya kwanza mwezi ujao.
4
Na Mwandishi Wetu -PEMBA UONGOZI wa Mkoa wa Kusini Pemba kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi umepongezwa kwa kuyabainisha na kuyarejesha serikalini mashamba ya Serikali na kuagiza kwa wale wote ambao bado wanayaficha wayarejeshe wenyewe kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria. Hayo yalisemwa jana Kisiwani Pemba na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ambapo alisema aliagiza kuchukuliwa hatua za kisheria bila kujali wadhifa wa mtu, cheo alichonacho au umaarufu wake. Agizo hilo alilitoa katika majumuisho ya ziara yake aliyoifanya kuanzia Agosti 24, mwaka huu ambapo aliwaagiza viongozi wa mikoa na wilaya kusimamia vizuri ukusanyaji mapato na kushirikiana na wafanyabiashara katika kuwashajiisha ili walipe kodi na kuongeza mapato ya Serikali. Aliwataka viongozi hao kutojiingiza katika kuwasaidia kukwepa kodi wala kuwakingia kifua kwa makosa yao wanayoyafanya katika kukwepa kulipa kodi. Pamoja na hali hiyo aliagiza Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo kufanya mkutano maalumu na wakuu wa mikoa na wilaya zote za Unguja na Pemba kwa ajili ya kupanga na kupeana majukumu ya utekelezaji wa mpango wa utalii kwa wote.
3
*Stand United yazidi kupeta, Coastal Union yazinduka NA WAANDISHI WETU MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga, jana waliendeleza ubabe katika ligi hiyo baada ya kuifanyia mauaji Toto Africans kwa kuifunga mabao 4-1 huku mahasimu wao, Simba wakilala kwa kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons. Ushindi wa jana kwa Yanga ambao wamecheza mara moja ugenini dhidi ya Mtibwa Sugar na kushinda mabao 2-0 Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, ni wa sita kwa vinara hao katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Matokeo hayo yameiwezesha Yanga kuendelea kutesa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo kwa kufikisha pointi 19 huku ikiwaacha kwa mbali watani wao wa jadi Simba ambao wameshuka hadi nafasi ya nne wakiwa na pointi 15. Stand United wamefanikiwa kufikisha pointi 15 sawa na Simba na kuishusha hadi nafasi ya nne baada ya jana kuifunga Majimaji ya Songea mabao 3-0 Uwanja wa Kambarage, Shinyanga lakini wakitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa. Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Elius Maguli, aliendeleza kasi yake ya kupachika mabao baada ya kuifungia timu yake mabao mawili dakika za 48 na 60 huku Pastory Pato akihitimisha kwa kufunga bao la tatu dakika ya 68. Simba wameshindwa kuishusha Yanga kileleni na kuwaacha katika upinzani mkali na Azam FC ambao wanatarajiwa kuvaana na Ndanda FC leo katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara. Yanga waliokuwa wenyeji wa Toto, walianza kwa kasi pambano hilo jana na kufanya shambulizi kali dakika ya kwanza kupitia kwa mshambualiaji wake, Amissi Tambwe, lakini shuti hafifu alilopiga akiunganisha pasi ya Juma Abdul liliokolewa kirahisi na kipa Musa Mohamed. Dakika ya nane Abdul alifanikiwa kuandika bao la kuongoza kwa Yanga baada ya kupiga shuti kali lililotinga nyavuni akiunganisha vyema mpira wa kona iliyochongwa na kiungo mchezeshaji, Haruna Niyonzima. Toto walijibu mapigo kwa kufanya shambulizi kali dakika ya tisa kupitia kwa Miraji Athumani aliyeachia shuti lililopitiliza moja kwa moja pembeni mwa lango la Yanga na kutoka nje. Mshambuliaji kinda wa Yanga, Godfrey Mwashiuya, alifanya uzembe na kukosa bao la wazi dakika ya 30 baada ya kutengeneza nafasi nzuri ya kufunga lakini akatoa pasi kwa Donald Ngoma na mpira kutua mikononi kwa kipa. Yanga walizidisha mashambulizi langoni kwa Toto na dakika ya 44 walipata penalti baada ya mchezaji, Karlos Protas wa Toto kushika mpira uliopigwa na Ngoma akiwa katika harakati za kuokoa. Hata hivyo, kipa Mohamed wa Toto alidhihirisha ubora wake baada ya kuidaka penalti hiyo iliyopigwa na Ngoma na kuwawadhibiti vilivyo Yanga kipindi cha kwanza licha ya kukabiliwa na tatizo la umaliziaji. Kiungo Simon Msuva aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Abdul, aliifungia Yanga bao la pili baada ya kuachia shuti la mbali akiwa nje ya eneo la 18 lililomshinda kipa wa Toto Hata hivyo, dakika ya 55, Japhet Vedastus wa Toto  aliifungia timu yake bao kwa mpira wa kichwa baada ya kutokea piga nikupige langoni kwa Yanga na kuwachanganya mabeki. Dakika ya 81, Tambwe aliongeza bao la tatu kwa Yanga baada ya kutumia makosa ya kizembe yaliyofanywa na mabeki wa Toto na kuachia shuti kali akiwa ndani ya eneo la hatari. Msuva alihitimisha karamu ya mabao kwa Yanga kwa kuandika bao la nne dakika ya 89 baada ya kufanikiwa kuunganisha vyema pasi ya Andrey Coutinho aliyeonyesha kiwango cha uhakika katika mchezo huo. Mwamuzi wa mchezo huo, Ahmada Simba wa Kagera, alimuonya kwa kadi ya pili ya njano na kumtoa nje Hassan Khatib wa Toto aliyemfanyia madhambi Haji Mwinyi wa Yanga. Kwa upande wa Simba waliokaribishwa na maafande wa Tanzania Prisons katika Uwanja wa Sokoine, Mbeya, walijikuta wakichezea kichapo cha bao 1-0 na kushindwa kufikia malengo yao ya kuondoka na pointi sita kwenye uwanja huo. Bao lililofungwa na Mohamed Mkopi dakika ya 61, lilitosha kuizamisha Simba na kuinyima pointi muhimu baada ya Jumamosi iliyopita kufanikiwa kuichapa Mbeya City bao 1-0 kwenye Uwanja huo. Coastal Union ambao wamemtimua rasmi kocha wao mkuu, Jackson Mayanja, ilizinduka katika ligi hiyo na kuichapa Kagera Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Bao la pekee na la ushindi kwa Coastal Union lilipachikwa wavuni na Ismail Mohamed dakika ya 13 akiunganisha krosi safi iliyochongwa na Ibrahim Twaha.                      
4
WAKATI Uchaguzi wa wabunge kwa ajili ya Bunge dogo la Rwanda ukitarajiwa kufanyika kwa siku nne kuanzia Septemba mosi mwaka huu, nchi hiyo inatarajiwa kuwa na idadi kubwa ya wanawake bungeni baada ya wanawake wengi kujitokeza kuwania uongozi. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema katika uchaguzi huo, kati ya wagombea 521 waliopitishwa, 326 ni wanawake ambayo ni sawa na asilimia 61 ukilinganisha na wanawake 221 walioshiriki mwaka 2013.“Tuna wagombea wengi wanawake, hii ni ishara nzuri kuwa wanawake wengi wamevutiwa kushiriki kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, haya ni maendeleo chanya,“ alisema Mwenyekiti wa NEC, Profesa Kalisa Mbanda. Wanawake 179 wanagombea nafasi 24 zilizotengwa kwa ajili ya viti maalumu huku vingine 147 wanashindana kupitia vyama vyao pamoja na nafasi kwa ajili ya vijana. Ikiwa ni mara ya kwanza baada ya mauaji ya halaiki kwa jamii ya Watutsi, chama cha upinzani wanashiriki katika sanduku la kupiga kura kwa kuwa na wagombea 32 kati ya 34 waliopendekezwa na chama cha Democratic Green (DGPR).Wagombea hao wameshiriki katika uchaguzi huo wa awamu ya nchi kushika nafasi mbalimbali. Kiongozi wa chama hicho, Frank Habineza alisema wanatarajia kupata angalau viti 10, kwa sababu ya mtandao walionao sasa nchi nzima na ukuu wa kisiasa waliopata baada ya kushiriki uchaguzi wa Rais uliopita ingawa walipata asilimia 0.5 dhidi ya Rais Paul Kagame aliyepata asilimia 98.8 katika uchaguzi wa Rais wa Agosti 2017. Mshindi wa pili katika uchaguzi wa rais kwa asilimia 0.7 ni kati ya wagombea binafsi wanne waliopitishwa na NEC kushiriki katika uchaguzi huo wa wabunge.Imeelezwa kuwa vijana 26 wanagombea nafasi mbili za vijana bungeni huku watu wenye ulemavu 10 wanagombea nafasi moja ya watu hao bungeni. Wabunge vijana Bunge linatarajiwa kuwa na mchanganyiko mkubwa wa vijana ambao wana wastani wa umri wa miaka kati ya 38 na 42. Lakini, Chama tawala RPF na chama mwenza, wagombea wake ni watu wazima wenye umri wa kati ya miaka 48 na 50, licha ya Rais Kagame kubainisha kuwa na vijana wengi katika nafasi za uongozi.Logan Ndahiro (67) na Fidele Rwigamba (68) ndio wenye umri mkubwa zaidi katika chama tawala cha RPF ambao pia wameonesha nia ya kutaka kutetea nafasi zao, wakati mwenye umri mdogo ana umri wa miaka 30. Wagombea 10 wa Chama cha Jamii na Demokrasia (PSD) wanaotarajia kushinda viti hivyo mkubwa ana miaka 48 na mwenye umri mdogo ni miaka 28 huku mtu mwenye umri mkubwa katika orodha ya Chama cha Liberal (PL) ana umri wa miaka 62 na kijana ana umri wa miaka 38.The Greens na PS Imberakuri kwa wastani wana umri wa miaka 38 huku wagombea wanne binafsi wakiwa na miaka 29 na 40 huku wagombea wanawake wakiwa na idadi kubwa ya wagombea vijana wengi wao wakiwa na miaka isiyozidi 40 na wagombea wote wa nafasi ya vijana wana umri chini ya miaka 30. Mwenyekiti wa NEC, Prof.Kalisa Mbanda alisema kwa ulinganifu, wagombea katika uchaguzi huo wana umri mdogo ukilinganisha na chaguzi zilizopita, hiyo inabainisha kuwa bunge lijalo litakuwa na wabunge wengi vijana. Alitoa mfano kuwa wagombea wote binafsi ni vijana na hata katika wagombea wa viti maalumu kwa wanawake wengi wao ni vijana. Zaidi ya raia wa nchi hiyo milioni saba wanatarajiwa kupiga kura katika uchaguzi huo utakaogharimu dola milioni 6.8. Bunge dogo nchini humo ina viti 80, kati yao 53 ni kwa ajili ya vyama vya siasa na wagombea binafsi, huku 24 ni kwa wanawake wanaochaguliwa.
3
TANZANIA imeanza maandalizi yake kuelekea mashindano ya Dunia ya mbio za nyika yanayotarajiwa kufanyika Machi 30 mwaka huu katika mji wa Aarhus, Denmark.Uchaguzi wa wanariadha watakaounda timu ya taifa ya mbio za nyika utafanyika mwishoni mwa wiki ijayo katika viwanja vya magereza mjini Moshi. Maandalizi ya kwanza ya mbio hizo za ‘Ngorongoro National Cross Country’ yalifanyika jijini hapa katika viwanja vya magereza na kushirikisha zaidi ya wanariadha 100 kutoka maeneo mbalimbali yalimalizika kwa wanariadha kutoka JKT na JWTZ kung’ara.Kwa upande wa wanaume waliokimbia kilomita 8 Stephano Huche aliongoza baada ya kutumia dakika 24:15: 53 akifuatika na Marco Silvester aliyemaliza kwa dakika 24:20:48 wote kutoka JKT huku kwa upande wa wanawake Cecilia Ginoka kutoka JWTZ alingoza kwa dakika 22:10:71 akifuatiwa na Angelina Tsere kutoka JKT kwa dakika 22:14:74.Akizungumzia maandalizi hayo katibu mkuu wa shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Wilhelm Gidabuday alisema mashindano hayo ya nyika ni maandalizi kuelekea mbio za Dunia na ni muhimu kwani yapo katika kalenda ya shirikisho.
4
HATIMAYE ndoto ya Mwalimu Julius Nyerere ya Watanzania kupata umeme kutoka Maporomoko ya Rufi ji inatimia, kwa leo Rais John Magufuli kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa bwawa.Rais Magufuli ambaye aliwasili Kisaki mkoani Morogoro jana, tayari kwa kazi hiyo anayoifanya leo, pia ametoboa siri ya kutumia usafiri wa treni kuja kuzindua mradi huo. Aidha, ametoa onyo la mwisho kwa viongozi wa Mkoa wa Morogoro kukomesha uhalifu unaofanywa na wafugaji dhidi ya wakulima.Rais Magufuli alisafiri kwa treni ya Tazara jana asubuhi kutoka Dar es Salaam hadi Kisaki mkoani Morogoro, kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa kufua umeme wa maji katika mto Rufiji. Uwekaji huo wa jiwe la msingi la mradi huo utakaofua megawati 2,115 utafanyika leo katika Pori la Akiba la Selous wilayani Rufiji mkoani Pwani. “Nimeamua kuja kwa treni makusudi.Nimetaka kutua hapa Kisaki kwa sababu ni mji unaokua kwa kasi sana,” alisema Rais Magufuli alipozungumza na mamia ya wananchi wa Kisaki alipofika jana mchana akiambatana na mkewe Mama Janeth.Aliwaambia wananchi hao kwamba kwa kujengwa mradi huo mkubwa wa umeme, Kisaki ichangamkie fursa za kujenga hoteli na nyumba za kulala wageni watakaokwenda Rufiji kuona utalii utakaotokana na mradi huo. “Chapeni kazi mfaidike na mradi huu. Mkienda kufanya kazi kule msiibe vifaa. Huu ni mwanzo tu wa mafanikio makubwa. Hapa mji wenu utabadilika sana,” alisema Rais Magufuli.Aliwageukia viongozi wa Mkoa wa Morogoro na kuwataka kukomesha matatizo ya wafugaji ambao wanavamia mashamba ya wakulima. “Natoa onyo la mwisho mkomeshe matatizo ya wafugaji.Nilikuja hapa na Rais wa Awamu ya Nne miaka minne sasa imepita. Tatizo halijaisha. Nataka mkomeshe hili tatizo. Likiendelea nitajua hamtoshi kuendelea kuwa viongozi,” Rais Magufuli alimwambia Mkuu wa Mkoa, Dk Stephen Kebwe na watendaji wake.Alisema wapo viongozi wanaohongwa wakiwamo polisi, hivyo akawataka wakikamata mifugo ipigwe mnada pamoja na kuwa na mahakama zinazotembea ili kuendesha mashitaka kwa wahalifu.Katika kuchangia maendeleo, Rais Magufuli alitoa Sh milioni 400 za kujenga kituo cha afya Kisaki. Pia aliendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo cha polisi ambazo zimepatikana Sh milioni 39.Ameagiza ujenzi huo uanze kesho na kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa, utadumu kwa miezi mitatu. Katika uwekaji jiwe la msingi la mradi wa kufua umeme wa maji wa Rufiji, maandalizi yake yamekamilika.Viongozi mbalimbali wa serikali, mabalozi na wananchi takribani 2,000 watahudhuria sherehe za leo wilayani Rufiji. Mradi huo unaojengwa na mkandarasi Kampuni ya ubia ya Arab Contractors na Elsewedy zote za Misri, una gharama ya Sh trilioni 6.5 za Watanzania wenyewe. Utakamilika Juni 2022.
3
  LAGOS, Nigeria CHAMA Cha Wanawake wanaofanya biashara ya kujiuza nchini  Nigeria, kimetishia kuitisha mgomo kwa kile ambacho kinadai kuwa wanachama wake wamekuwa wakilazimishwa kufanya ngono na polisi  baada ya kuwakamata na kuwatishia kuwafungulia mashtaka. Chama  hicho kilisema juzi kuwa asilimia 50 ya wanachama wake wamekuwa wakifanyiwa  vitendo hivyo na polisi katika mji wa Anambra  katika Jimbo la Orumba Kusini. Mmoja wa wanawake ambaye alijitaja kwa jina moja la  Kaamsi, ambaye pia ni mmoja wa viongozi wa chama cha  Orumba South LGA,  alisema  polisi wamekuwa wakiwafuata katika maeneo yao na kuwabughudhi kabla ya kuwalazimisha kulala nao. “Polisi hawa wameshawalazimisha asilimia 50 ya wanachama wetu, wamekuwa wakija katika maeneo yetu na kutumbua kila siku.” alisema kiongozi huyo. “Karibu siku mbili zilizopita  hapa  hakuna wanachama  chini ya 10  kwa sababu  walikamatwa na kupelekwa kwenye ofisi  za polisi. Walikuwa wakitendewa vibaya…. kabla ya kuruhusiwa walilazimishwa kulipa dhamana kwa kutumia miili yao,”aliongeza kiongozi huyo. Alisema   matukio hayo yamekuwa yakitokea kila siku katika maeneo ya  Umunze, Onitsha, Awka, Nnewi, Ekwulobia na kwamba wamekubaliana hakuna mwanachama yeyote atakayempa huduma polisi katika eneo hilo la  Umunze na mengine katika jimbo hilo. Alipohojiwa kama askari hao wamekuwa  wakivaa sare  za kazi,  Kamsi alisema   wanawatambua kwa vile  wanamfahamu kila mteja wao na siyo lazima wawe na sare ndiyo wawatambue.
2
LONDON, UINGEREZA NCHI za kusini mwa jangwa la Sahara zimeimarisha kampeni ya kuondoa adhabu ya kifo baada ya kuchangia katika kupungua kwa utekelezaji wa adhabu hiyo duniani, kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Haki za Binadamu, Amnesty International. Rpoti hiyo iliyotangazwa jana ilisema kuna mwenendo mzuri unaoendelea duniani, ambapo matukio ya watu kunyongwa yalipungua kwa asilimia nne kutoka watu 1,032 hadi 993 mwaka jana. Guinea ilifuta adhabu ya kifo kwa makosa yote ya uhalifu, wakati Kenya haitoi tena hukumu ya kifo iliyokuwa ya lazima kwa kosa la mauaji. Burkina Faso imesifiwa na Amnesty kwa rasimu yake ya katiba ambayo inajumuisha kipengele cha kuondoa kabisa adhabu ya kifo. Aidha Chad kwa kuanzisha sheria mpya ambayo inaruhusu tu hukumu ya aina hiyo katika kesi ya ugaidi. Nchi 20 katika eneo hilo zimeondoa adhabu ya kifo kwa makosa yote ya uhalifu, huku Somalia na Sudan Kusini zikiwa nchi pekee zilizotekeleza adhabu hiyo mwaka jana ikilinganishwa na mataifa matano katika mwaka 2016.
2
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi (pichani) amefi chua jinsi watumishi 183 wa ardhi walivyoingia kwenye ufi - sadi wa kuikosesha serikali mabilioni ya fedha, huku akimuagiza Katibu Mkuu wake kuunda timu ya wataalamu kuchunguza zaidi watumishi hao waliosimamishwa.Wakati akisema timu hiyo itaanza kazi Jumanne ijayo kwa siku 30, amesema watumishi hao walishiriki ama kupunguza au kufuta madai ya kodi kwa baadhi ya wananchi; ikiwamo viwanja viwili vya Hoteli ya Mbeya vyenye ukubwa wa mita za mraba 20,234 huku kwenye mfumo vikiandikwa mita za mraba 5.2, jambo lilimfanya mmiliki huyo kutolipa kodi ya zaidi ya Sh milioni 68.Lukuvi aliyasema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana jijini hapa, kufafanua hatua ya kuwasimamisha kazi watumishi wa ardhi 183 kutoka wizarani na katika halmashauri mbali mbali nchini, waliobainika kuingilia mfumo wa malipo ya kodi, kwa ama kufuta kodi anayodaiwa mtu au kupunguza kiwango cha kodi.Timu ya Wataalamu Alisema timu hiyo itakayojumuisha wajumbe kutoka vyombo vyote vya kiuchunguzi nchini, wataalamu wa teknolojia ya mawasiliano (IT) kutoka wizarani na wale wa mfumo wa malipo wa serikali, itakayoongozwa na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), itatakiwa kufanya uchunguzi wa mfumo wa kodi wa wizara kuanzia mwaka 2016 ambapo mfumo huo ulianza kazi.“Timu pia inatakiwa kupitia mfumo wa kodi wa wizara kuangalia kama ni mtimilifu, na pia kupitia taarifa za watu wote na mfumo kuanzia mwaka 2016 tangu wizara ijiunge na mfumo wa malipo wa serikali na kama kuna watakaobainika basi wachukuliwe hatua za kinidhamu kama mtumishi na kisheria kwa kufikishwa mahakamani. Hivyo uchunguzi huu utahusiska miaka mitatu,” alieleza Lukuvi.Mchezo mzima ulivyokuwaAkifafanua, Lukuvi alisema watumishi waliosimamishwa ni wale waliobainika kuingia kwenye mfumo na kufuta au kupunguza ankara za kodi, ambazo wananchi wanadaiwa kama kodi ya viwanja, huku fedha hizo zikiwa hazionekani kulipwa au kulipwa kidogo kwenye mfumo wa malipo wa serikali.“Mwananchi aliyepewa hati na kumilikishwa ardhi haingizwi kwenye mfumo wa ulipaji wa kodi wa wizara, kwanza kuna mfumo wa wizarani ambao unaorodhesha wamiliki wote waliomilikishwa ardhi kwa matumizi mbali mbali, na mfumo huu unaweka kumbukumbu ya kiwango cha mtu anachotakiwa kulipa kila mwaka. “Kila unapolipa mfumo huu hujirekebisha wenyewe kwa kufuta deni na kama hujalipa baada ya miezi sita unaongeza kwa kulipa penalti, na ulipaji wa kodi ya ardhi unaanza Julai Mosi kila mwaka, na hizi vyote kumbukumbu zinakuwa kwenye mfumo wa kodi wa wizara,” alisema Lukuvi.Alisema hatua hiyo ilifikiwa baada ya wizara kuingiwa na shaka juu ya uendeshwaji wa mfumo huo na kuamua kufanya uchunguzi kwa kipindi cha miezi sita ya mwaka wa fedha 2018/2019.Jinsi wizara ilivyogunduaAkifafanua walichokibaini, alisema watumishi hao wenye dhamana ya kudhibiti mfumo wa malipo katika wilaya zao, walibainika kuingilia mfumo huo na kusababisha taarifa za malipo zilizopo katika mfumo wa wizara na ule malipo ya serikali uliopo Hazina wa GePG, kutooana na kubaini kuna baadhi ya wadaiwa ama hawakulipa kabisa au wamelipa kidogo ukilinganisha na deni halisi.“Katika kila wilaya tuna mtu mmoja aliyepewa password (neno la siri) la kuingia kwenye mfumo kuingiza kiwango cha kodi na kudhibiti na kuonesha nani anatakiwa kulipa kodi ndani ya wilaya, hivyo kila wilaya inayo kumbukumbu ya wamiliki na kiasi gani cha kodi wanadaiwa. “Tulipofuatilia mfumo wetu na tunajua baadhi ya watu fulani wanadaiwa kiasi gani na tulipolinganisha na mfumo wa GePG ambao unapokea fedha za serikali kule Hazina, fedha zilizopokelewa kutoka kwa wadaiwa ni kidogo ukilinganisha kiwango kilichofundwa kwenye mfumo wa kodi wa wizara,” alisema Lukuvi.Aliongeza: “Mfumo wetu unaonesha nani aimeingia kwenye mfumo, nani ameandaa invoice ndogo iliyomwezesha mwenye kiwanja kulipa fedha kidogo Hazina na baadaye nani ameingia na kufuta deni lote kwenye mfumo.”“Tulichogundua ni kuwa ingawa kwenye mfumo wa wizara mwenye kiwanja A anadaiwa shilingi milioni 3 na kwenye mfumo wa wizara umefuta milioni 30 kana kwamba huyu mdaiwa amelipa fedha zate, lakini mapokezi ya pili kwenye mfumo wa Hazina huyu mtu amelipa shilingi milioni 3. Kwa hiyo, tumegundua tofauti kati ya fedha halisi zilizopokelwa na kiwango cha fedha na data zilizofutwa,” alibainisha waziri huyo.Alisema watumishi 183 waliosimamishwa kazi ni wale tu ambao wameonekana kuingilia mfumo ndani ya kipindi cha miezi sita ; na kuonekana kupunguza au kufuta kiwango cha kuanzia Sh 100,000 na kuendelea.Waliofutiwa madeni wako salama?Hivyo, alisema wananchi wote waliofutiwa, kupunguziwa madeni yao ya kodi za viwanja, madeni hayo yako palepale na watachukuliwa hatua za kisheria kwa kushiriki kuiibia serikali kwa kushirikiana na watumishi wa ardhi.“Nataka niwaambie na wale wananchi ambao wanafikri wamefutiwa madeni yao kwa utaratibu huu, nao hawako salama, kwa maana nao watahusika wamehusika katika kuiibia serikali. Umefanya makusudi kupata na afisa ardhi kupunguziwa deni na kumlipba bila risiti, huo ni wizi wa makusudi. Watu wote ni wajanja huko pengine majina ao yamefuta, hajafutwa nao hawako salama,” alisema.Udanganyifu mwingine Aidha, alisema mbali na hujuma ya mapato ya serikali, pia baadhi ya watumishi wa sekta hiyo wamekuwa wakifanya udanganyifu kwa kupunguza ukubwa la eneo analomiliki mtu ili kumfanya alipe fedha kidogo.“Kumekuwa na wizi huo ambao unafanywa na maofisa ardhi ambapo kama mwananchi ana kiwanja cha square mita 10 anapunguziwa na kubakiziwa square mita 500 hivyo anailipa serikali kiasi kidogo ilihali anamiliki eneo kubwa na kuisababishia serikali kukosa mapato,” alieleza.Akitoa mfano, alisema kuna mtu alibinafsishiwa kiwanja namba 1 na 2 katika kitalu 1 cha Mbeya Hotel kilichopo Uzunguni jijini Mbeya, chenye ukubwa wa mita za mraba 20,234 kuanzia mwaka 2002, lakini ofisa ardhi aliamua kumpunguzia eneo hilo na kuingiza kwenye mfumo kuwa kodi ya kiwanja kina ukubwa mita za mraba 502.Alisema kwa ukubwa mita za mraba 20, 234, mmiliki huyo alipaswa kulipa kodi ya shilingi 6,373,804.50 kwa mwaka, lakini kutokana na kupelekewa ukubwa mdogo, analipa kodi ya shilingi 63,252 hivyo kufanya mmiliki huyo kukwepa kiasi cha shilingi 68.406,138 (zaidi ya shilingi milioni 68.4) kwa kipindi chote hicho miaka 17.“Huyu kijana aliyehusika na jambo hili kama yupo ndani ya serikali, Katibu Mkuu atashughulika naye na nimeshampa jina, na yupo ndani ya wizara na ameikosesha serikali zaidi ya shilingi milioni 68,” alisema.Alitumia fursa hiyo kuwatoa shaka wananchi kuwa hatua ya kusimamisha watumishi hao 183, hakutadhoofisha utendaji katika sekta ya ardhi, kwa sababu tayari imeshachukua hatua ya namna bora ya kuwahudumia wananchi.“Tumeshajua waliobaki katika sekta hii, wajue kuwa mbinu zao zinajulikana na walikuwa wanafuja na kushirikiana na watu wa idara yangu, sasa wako wizara,” alisema Lukuvi.Ushauri kwa wananchi Aliwataka wananchi kutoenda ofisi za ardhi, kujua kile wanachodaiwa au kulipa kodi zao, bali wanaweza kufanya hivyo kwa kulipia benki au kwa njia ya simu za mkononi.“Mwananchi huhitaji kumfuata ofisa ardhi kukaa mezani na kufanya mazungumzo maana hivi sasa wizara imerahisisha huduma za malipo ikiwemo kwa njia ya simu na wakala wa benki hivyo wanaweza kulipa ankara bila wasiwasi na bila kwenda kumuona ofisa ardhi ofisini,” alisema.Kuhusu mapato, alisema kwa mwezi mmoja, serikali imepokea malimbikizo wa madeni ya kodi kutoka kwenye wizara, taasisi za umma na kampuni kiasi cha Sh bilioni 21 na kusisitiza kuwa kwa sasa wizara yake inaendelea na kampeni ya wananchi kulipa kodi kwa hiyari.
3
KOCHA wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars Emmanuel Amunike ametangaza kikosi cha wachezaji 25 kitakachoingia kambini kufanya maandalizi ya kuvaana na Uganda kwenye mchezo wa mwisho wa kuwania kufuzu fainali za mataifa Afrika ‘Afcon’.Mchezo huo unatarajiwa kupigwa nchini Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa ambapo kwa Tanzania inahitaji ushindi ili kufuzu fainali hizo zinazotarajiwa kufanyika Misri. Katika mchezo wa awali uliofanyika Kampala, Stars ililazimisha suluhu. Katika kikosi kilichotangazwa jana, Amunike hakumwita Abdi Banda anayecheza FC Baroka ya Afrika Kusini.Banda alikuwepo kwenye kikosi kilichocheza na Uganda na Lesotho. Mbali na hao, wachezaji wanaocheza nchini na kufanya vizuri kwenye timu zao kama Ibrahim Ajibu wa Yanga na Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jnr’ wa Simba hawajaitwa kikosini. Akilizungumzia hilo, Amunike alisema timu ya taifa si mali ya mtu hivyo kila mchezaji anastahili kuitwa. Kikosi kilichotajwa jana ni Aishi Manula, John Bocco na Jonas Mkude (Simba ), Mechata Mnata, Vincent Philipo, (Mbao FC), Aaron Klambo (Mbeya City) Sulemani Salula( Malindi FC).Aggrey Moris, Mudathir Yahaya (Azam FC), Feisal Salum, Kelvin Yondani, Michael Gadiel, (Yanga), Himid Mao ( Petrojet-Misri) Yahya Zaydi (Ismailia- Misri), Hassan Kessy (Nkana Rangers- Zambia), Ally Mtoni (Lipuli FC). Wengine ni Shaaban Chilunda, (Tenerif- Hispania),Shiza Kichuya,( Enppi SC- Misri), Simon Msuva (Difaa El Jadidi- Morocco), Rashid Mandawa (BDF XI- Botswana) ,Mbwana Samatta ( KRC Genk- Ubelgiji), Thomas Ulimwengu (Js Saoura- Algeria), Farid Mussa (Tenerife- Hispania).“Tunawachezaji wengi lakini wachezaji niliowatangaza nadhani watajituma kuhakikisha wanapigania taifa lao kwa moyo wote na kwa wasiochaguliwa wasijisikie vibaya watapata nafasi wakati mwingine,” alisema Amunike.Alisema Uganda wameshafuzu lakini anaamini mchezo utakuwa mgumu kwani hawatahitaji kupoteza hivyo amechagua wachezaji ambao ameangalia uwezo wao na wataipatia nchi matokeo. Alisema, timu inatarajiwa kuingia kambini muda wowote na kwa wachezaji wanaocheza nje ya nchi wanatarajiwa kuwasili kuanzia Machi 17. Kwa upande wa wapinzani wao, Uganda tayari wameweka kambi Misri tangu juzi kujiandaa na mechi hiyo inayotarajiwa kuwa ya vuta nikuvute.
4
Na Gurian Adolf-Sumbawanga JESHI la Polisi mkoani Rukwa linawasaka watu wasiojulikana kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga mawe, Maria Birika(40) mkazi wa Kijiji cha Myunga,wilayani Kalambo akituhumiwa kujihusisha na vitendo vya kishirikina. Tukio la mauaji ya Maria lilitokea Juni 26, mwaka huu  saa 12:00 jioni, baada ya watu watuhumiwa kufika nyumbani kwa Maria na kukumkuta mtoto Given Lameck, akiwa amefungiwa nyumbani kwa mwanamke huyo, huku akiwa amefungwa kitambaa chekundu usoni. Kabla ya mauaji hayo, Given alipotea nyumbani kwao katika mazingira ya kutatanisha, ndipo harakati za kumtafuta zilipoanza ambapo ndugu zake walimtafuta muda mrefu bila mafanikio. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Justine Masejo alisema baada ya jitihada za kumpata mtoto kugongwa mwamba, waliamua kutoa taarifa kwenye uongozi wa kijiji kuhusu tukio la kupotea kwa mtoto,kisha kuendelea kumtafuta. Alisema  baada ya kumtafuta muda mrefu, walifanikiwa kumkuta nyumbani kwa Maria akiwa amefungiwa ndani na amefungwa kitambaa chekundu usoni, huku akionekana amechanganyikiwa kutokana na kuzungumza vitu visivyo eleweka. Baada ya kupatikana mtoto,ndipo watu waliokuwa wakimtafuta walihamaki na kushikwa na hasira na kuanza kumpiga Maria  kwa mawe na vipande vya matofali vilivyokuwa karibu na nyumba yake na kumsababishia majeraha makubwa,kuvuja damu nyingi na kufariki dunia kutokana na kukosa matibabu ya haraka. Kamanda Masejo alitoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kuachana na imani za kishirikina katika matukio yanayotokea mkoani humo,kwani imani hizo zimekuwa chanzo cha vifo vingi na sababu ya kujichukulia sheria mikononi.
0
Mwandishi wetu, Tanga WAFANYABIASHARA wa Mkoa wa Tanga, wamesema hawaoni shidakulipa kodi baada ya kuona utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleoinayofanywa na Rais Dk. John Magufuli kupitia kodi zao. Hayo yalizungumzwa na wafanyabiashara wakati wa kampeni ya elimukwa mlipakodi inayoendelea mkoani humo ambako maafisa wa Mamlakaya Mapato Tanzania (TRA) kutoka Makao Makuu kwa kukishirikiana namaafisa wa TRA mkoa wa Tanga. Maafisa hao waliwatembelea wafanyabiashara kwenye maduka yaoyaliyopo barabara za namba jijini Tanga kwa lengo la kuwaelimisha nakuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati.Sambamba na hilo, maafisa hao pia waliweza kusikiliza kerozinazowakabili wafanyabiashara mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusikiliza maoni yao kama mpango wa kutengeneza mazingira rafiki kati yao naTRA.Thabiti Salimu ambaye ni mfanyabiashara wa Ukwaju wa jumla na rejarejakatika eneo la barabara za namba amesema kuwa, atamshangaamfanyabiashara atayekwepa kulipa kodi hususani katika kipindi hikiambacho wameshuhudia miradi mingi ikitekelezwa kupitia kodi zao. “Rais Magufuli anatumia kodi zetu vizuri, tunaona utekelezaji wa miradimingi ya maendeleo hivyo lazima tuendelee kulipa kodi la sivyo kazi yautekelezaji wa miradi hii itakwama,” alisema Salimu. Naye Dina Mbenu, mfanyabiashara wa vipuli vya pikipiki amesema kuwa,ikiwa wafanyabiashara watakwepa kulipa kodi watasababisha madhara yakiuchumi na kuathiri jitihada za serikali za kuboresha miundombinuikiwemo barabara. Amesema hatua ya maafisa wa TRA kuwatembelea kwenye maduka yaokwa lengo la kuwahamasisha kulipa kodi na kusikiliza kero na maoni yaoinawasaidia kutopoteza muda kwenye ofisi za TRA wakisubiri kuhudumiwa. Kwa upande wake Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi Julius Mjenga amesemazoezi la kuwatembelea wafanyabiashara ni endelevu na kabla ya kufanyikaTanga, zoezi hilo limeshafanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza,Mbeya na Morogoro. Amesema lengo la kufanya hivyo ni kutoa elimu ya kodi, kuwakumbushawafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati, kusikiliza maoni yao pamoja nachangamoto kwa ajili ya kuzitatua.Naye Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure, aliwaombawafanyabiashara kuunga mkono zoezi linalofanywa na maafisa wa TRA lautoaji elimu ya kodi, kusikiliza maoni na changamoto zao kwa kuwa zoezi hilo linalenga kuboresha huduma kwa mlipakodi.“Niwaombe wafanyabiashara wote mkiwaona maafisa wanatembelea,msifunge maduka, wapokeeni na kuwapa ushirikiano kwa kuwa wanalengakuwaelimisha na kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili kwenyebiashara zenu ambazo kwa pamoja tunaweza kuzitafutia ufumbuzi,”alisema Owure. Amesema zoezi hilo la utoaji wa elimu ya kodi kwa wafanyabiasharamkoani humo linatarajiwa kumalizika Juni 30, 2020 na kwamba lengo likiwani kutaka kuwafikia wafanyabiashara wengi mkoani hapo.
5
Droo hiyo iliyosimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini iliendeshwa mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.Akizungumza mara tu baada ya droo hiyo, Meneja bidhaa wa benki hiyo, Aloyce Maro alisema kampeni hiyo ni sehemu ya jitahada za benki hiyo kuwapatia wateja wake faida zaidi na huduma bora.Alisema kwa kuanzia, washindi wa droo hiyo walifanikiwa kujitwalia zawadi za simu za kisasa aina ya iPhone 6.“Pamoja na kutoa shukrani zetu kwa wateja wetu kutokana na mafanikio tunayoendelea kuyapata ni vema pia tuwe mrejesho wa mafanikio haya kwao pia. Ni katika mazingira hayo ndio maana tumekuwa na utaratibu wa kutoa zawadi kwa wateja wetu ili kufurahi pamoja,’’ alisema.Zaidi Maro aliwakumbusha wateja wa benki kuendelea kushiriki zaidi kwenye kampeni hiyo kwa kuwa bado wana nafasi zaidi ya kujishindia zawadi mbalimbali, ikiwemo zawadi ya gari kwenye droo tano zilizosalia.Sambamba na zawadi hizo Maro aliongeza kuwa kampeni hiyo inatoa riba nzuri zaidi kwa wateja wanaofungua akaunti hiyo ya malengo.
5
Na FARAJA MASINDE-DAR ES SALAAM UTAFITI mpya wa 36 uliotolewa na Taasisi ya Utafiti ya Twaweza Dar es Salaam jana, umewachambua Rais Dk. John Magufuli na vyama vya CCM na Chadema. Kwa mujibu wa utafiti huo uliotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, idadi ya wanaomuunga mkono Rais Magufuli imeshuka kutoka asilimia 96 mwaka jana hadi asilimia 71, mwaka huu. Pia, utafiti huo umeonyesha kuwa CCM inakubalika zaidi kwa wazee na watu wasiokuwa na elimu, huku Chadema ikiungwa mkono na wasomi, vijana, wanaume, matajiri na wenye elimu ya kutosha. Kwa mujibu wa Eyakuze, utafiti huo uligusa mambo tisa na kupewa jina la ‘Matarajio na matokeo, vipaumbele, utendaji na siasa nchini Tanzania’. “Tumeshuhudia pia uwepo wa kundi ambalo halikukubali wala kukataa utendaji wa Rais ambao ni asilimia 29 kutoka asilimia nne za mwaka jana, huku asilimia tisa wakisema hawamkubali. “Takwimu zinaonyesha kwamba pengo kubwa la kukubalika kwa Rais Magufuli linaonekana katika makundi ya rika mbalimbali, kwani asilimia 68 ni wenye umri chini ya miaka 30 ikilinganishwa na asilimia 82 ya wenye umri zaidi ya miaka 50,” alisema Eyakuze. Eneo jingine lililoguswa na utafiti huo ni vyama vya siasa ambalo asilimia 63 walisema wapo karibu zaidi na CCM, huku Chadema kikiwa na asilimia 17. “Utafiti unaonyesha kuwa CCM inakubalika zaidi miongoni mwa wazee kwa asilimia 80, ikilinganishwa na asilimia 55 za vijana na kwa upande  wa wanawake inakubalika kwa asilimia 68 ikilinganishwa na wanaume wanaoikubali kwa asilimia 58,” alisema. Kuhusu Chadema, Eyakuze alisema chama hicho kinakubalika zaidi miongoni mwa wanaume, vijana, matajiri na wenye kiwango kikubwa cha elimu. “Lakini, pale CCM inapoungwa mkono kwa kiwango kidogo, haimaanishi moja kwa moja kuwa Chadema inaungwa mkono kwa kiwango kikubwa,” alisema. Naye Waziri Mkuu mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, aliwapongeza Twaweza kwa utafiti huo, huku akiitaka Serikali na wawakilishi wa vyama kutilia mkazo suala la upungufu wa chakula. “Hongereni Twaweza kwa utafiti huu, lakini si kila kitu kilichoandikwa mle ni sahihi. Lakini kilichomo kinaakisi hali halisi ilivyo sasa,” alisema Dk. Salim. “Kuhusu suala la upungufu wa chakula, kama linatokana na mambo ya uwezeshaji, basi linatakiwa kupewa umuhimu wa aina yake kwa masilahi ya wananchi,” alisema Dk. Salim.
3
SERIKALI imebatilisha uamuzi wa kuwaondoa wanafunzi 48 wa shule za vipaji maalumu ambao walipata daraja la tatu katika mtihani wa ndani wa muhula wa pili wa kidato cha sita kwenda shule za bweni za kawaida baada ya kupoteza nafasi ya kuendelea na masomo kwenye shule hizo.Waziri wa Nchi , Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa kwenye ziara katika shule ya Sekondari ya Kilakala ya wasichana wenye vipaji maalumu iliyopo mkoani Morogoro.“leo (Julai 19 , 2019) nitoe tangazo la wazi kwa wanafunzi wote 48 , kuwa Serikali imefanya tathimini imeona wanafunzi wote hao waendelee na masomo yao kwenye shule hizo kwa mpango maalumu… haya ndiyo matunda ya Serikali inayowajali watu wote,” alisema Jafo.Alisema Tamisemi kupitia wataalamu wake walitoa barua kwenda kwa Makatibu Tawala wa mikoa ya Tanzania Bara ikiagiza juu ya uhamisho wa wanafunzi waliopata daraja la tatu hadi sifuri .Wanafunzi hao waliopata madaraja hayo katika mitihani ya muhula wa pili ya kidato cha sita kwenye shule za Sekondari za Vipaji maalum kuwahamisha kwenda katika shule za Serikali za bweni za kawaida.“Siku za hivi karibuni wataalamu wangu walitoa maelekezo kwenye shule za vipaji maalumu kwa waliopata daraja la tatu hadi ziro wanatakiwa wahamishwe kwenda shule za serikali za bweni za kawaida na kubakia waliopata daraja la kwanza na la pili,” alisema Waziri Jafo.Alisema serikali imetafakari na imeona wanafunzi hao 48 waliopaswa kuondolewa waendelee kubaki kwenye shule hizo.Hata hivyo alisema wanafunzi hao wametakiwa waongeze juhudi kubwa za kusoma na wakuu wa shule hizo pamoja walimu wao kuandaa mpango mkakati wa kuwawezesha kufanya vyema katika masomo yao.Waziri Jafo alisema hayo ni maelekezo maalumu ya serikali na kwamba wanafunzi hao na wengine wahatakiwi kubweteka ila wanapaswa kujitambua kuwa kuchaguliwa kwenye shule za vipaji maalumu haikuwa ni kwa bahati mbaya isipo kuwa ufauli wao ni kiwango cha juu na unapaswa kuendelezwa wanapokuwa kwenye shule hizo.“Wanafunzi hawa wajiwekeee utaratibu wa kusoma kwa juhudi kubwa na walimu wa masomo yao waandae vipindi vitakavyowawezesha kufanya vyema sawa na wengine kupata alama za juu ,” alisema Jafo.Alisema lengo la serikali ni kuona matokeo ya mtihani mwaka 2020 shule zake zisizopungua sita zinaingia kumi bora na hilo litawezekana iwapo wanafunzi watazingatia masomo pamoja na wakuu wa shule kuweka programu maalumu zitakazosimamiwa na walimu ili kuwezesha ufaulu wa daraja la kwanza.Jafo alisema shule za sekondari za kata hasa zenye kidato cha sita zina kuja kwa kasi kubwa na kati ya Shule 100 bora , shule 52 kati ya 64 za serikiali ni za Kata jambo ambalo linazitishia Shule 12 za vipaji maalumu.
3
WAKATI fulani mwaka 2014, nikiwa kwenye semina yangu ya JS Love Talk iliyofanyika Sinza, jijini Dar es Salaam,  dada mmoja alisimama na kuuliza swali. Alikuwa akizungumza kwa uchungu huku akimwaga machozi. Alikuwa kwenye maumivu makali ya kuachwa na mpenzi wake wa muda mrefu. Ni mwanaume ambaye alikuwa naye mapenzini kwa muda wa miaka mitatu. Walifahamiana kwenye mtandao (Facebook), kila mmoja akajieleza kwa mwenzake na wote wakakubaliana kuwa wapenzi. Anasema mpenzi wake huyo anaishi na kufanya kazi mjini Iringa, wakati yeye akiwa hapa jijini Dar es Salaam. Walifanyiana mengi kwenye mapenzi yao. Wakawa na ahadi kedekede. Tatizo ni siku au tuseme wiki waliyokaa pamoja na kufahamiana. Dada huyo alikwenda Iringa kumuona mpenzi wake huyo kwa mara ya kwanza, lakini hakujua kuonana kwao ndiyo ilikuwa mwisho wa penzi lao. Anasema: “Alinipokea vizuri sana. Akanipeleka nyumbani kwake Kihesa. Lakini hakuonekana kufurahia sana ujio wangu. “Nililala naye na ilikuwa siku yangu ya kwanza kukutana naye kimwili. Akawa anaondoka asubuhi sana na kwenda kazini, kisha anarudi usiku wa saa tano wakati mwingine mpaka sita. “Sikupata muda mwingi wa kuwa naye, baada ya siku tano nilirudi Dar nikiwa sijamjua vizuri yule bwana. Kutokea hapo, kila nikimpigia simu hapokei, nikimtumia meseji hajibu. “Baadaye akanijibu kwa kifupi; kama hujui kusoma, hata picha huwezi kutazama? Sitaki mazoea tena na wewe, maana wewe siyo type yangu. Tangu hapo akawa hapokei tena simu yangu. “Najua hanitaki tena, lakini bado nampenda sana, nashindwa kumuondoa kichwani mwangu, nimechanganyikiwa sana. Naomba msaada wako mwalimu.” Nilizungumza naye pale, lakini pia baadaye nilizungumza naye zaidi chemba. Lakini kifupi niseme tu, mwanzo wa matatizo yote ni mapenzi ya kudanganyana kabla ya kuonana. Wakati naanza mada hii wiki iliyopita, nilieleza kwa kifupi namna hali inavyokuwa wakati wa kuanzisha uhusiano wa kabla ya kuonana. Hebu sasa tumalizie mada yetu, nikiamini kuwa mfano nilioanza nao hapo juu umekusaidia kukuongezea ufahamu.   MAPENZI YA HISIA Kimsingi sababu ya haya yote ni hisia tu. Njia ya mawasiliano inaweza kukoleza au kuimarisha uhusiano ambao tayari upo. Mfano kama unaishi Moshi na mpenzi wako yupo Mwanza, mnaweza kuboresha uhusiano wenu kwa kuwasiliana kwa njia ya simu, waraka pepe na mitandao ya kijamii. Kinachotokea kwa marafiki wapya ambao wanahisi tayari ni wapenzi na wanapendana ni zile hisia za ndani zinazowaingia wakati wa mawasiliano yao. Pengine walianza kuzungumzia mambo ya mapenzi na kujikuta wakitamani kuwa karibu. Jambo kubwa zaidi ni kwamba mhusika hutawaliwa zaidi na hisia, maana kwa sababu hawafahamiani, watakuwa wanauliza; ‘Wewe ukoje? Mrefu, mfupi, mwembamba, mnene au?’ halafu mwenzake atamjibu, ‘mrefu kiasi, si mnene sana, kifupi nina umbo namba nane…navutia na ni maji ya kunde’. Kifupi mtu anaweza kujielezea vyovyote atakavyo, hivyo kumfanya mwenzake amtengeneze ajuavyo kichwani mwake na kujihakikishia kwamba anampenda kwa dhati mwenzake kumbe anajidanganya!    TABIA BANDIA Mbaya zaidi ni kwamba, wakati wapenzi hawa wanaojidanganya wakiendelea kuwasiliana si rahisi kujuana vizuri kitabia kwa sababu wengi huonesha tabia bandia. Mambo yao ya ndani wanayaficha kwa nguvu na kuonesha mema tu. Hapo ndipo mwanzo wa penzi feki kwa kudanganyika na tabia za kutengeneza.   HULKA MBAYA Kuna wengine ni tabia zao za asili. Amezoea kupata wapenzi kwa kupitia kwenye simu na mitandao ya kijamii. Usishangae kuna wengine wanapiga namba hata wasizozijua, akikutana na mtu wa jinsia tofauti na yake, anaanza mambo yake. Akimaliza haja zake anakuacha!   ACHA KUJIDANGANYA Ni vizuri sasa ukatoka kwenye ulimwengu wa giza na kurudi kwenye ulimwengu unaonekana. Kwa hakika ni vigumu sana kumpenda mtu ambaye hujamuona, labda kama unataka kucheza na muda wako. Wako anakuja, vuta subira ukifanya mambo yako kwa usahihi. Usijidanganye na matapeli wa mapenzi. Wapo ambao baadhi ambao wanafanikiwa kuingia kwenye mapenzi lakini mwisho wao hauwi wenye mafanikio. Penzi la dhati hubebwa na vitu vingi sana, ukiachana na UPENDO kuna suala la tabia na mengine mengi ambayo huwezi kuyajua kwa njia ya kuwasiliana pekee. Utajihakikisha umempenda kwa kumtengeneza kichwani mwako, mwisho wa siku unakutana na mtu ambaye yupo tofauti na mawazo yako, itakuwaje hapo? Fikiri zaidi. Je, unapenda kujifunza masomo haya zaidi kupitia group la WhatsApp la Love Moment? Kama ndivyo karibu inbox, andika ujumbe wako ukitaka kujiunga na kundi hilo, nasi tutakuunganisha.
1
Katika mchezo wa kwanza ugenini Uwanja wa George V, Yanga ilishinda bao 1-0, matokeo ambayo yanawapa Yanga kazi nyepesi leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutinga hatua inayofuata kwani inahitaji angalau sare.Kocha wa Yanga, Mholanzi Hans van der Pluijm, amejitapa kushinda mchezo huo baada ya maandalizi mazuri waliyofanya kwa wiki mbili tangu warejee nchini.Pluijm ambaye katika mchezo huo atawakosa nyota watatu wakiwemo wawili wa kimataifa, Haruna Niyonzima na mfungaji wa bao pekee lililowapa ushindi ugenini Donald Ngoma, alisema pamoja na kuhitaji sare, lakini lazima washinde.“Tumejiandaa vizuri kuhakikisha tunashinda mchezo wa kesho (leo), kwa sababu tumefanya maandalizi ya kutosha na tunacheza nyumbani mbele ya mashabiki wetu hatutapenda kuwaangusha na kizuri zaidi tunawajua vizuri wapinzani wetu,”alisema Pluijm.Pluijm alisema pamoja na kuwakosa nyota hao, lakini ana imani kubwa na wachezaji waliopo ambao ana hakika watacheza kwa kiwango cha juu na kuwapa ushindi. Wapinzania wa Yanga, Cercle de Joachim, tayari wametua Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo huo huku wakionekana wamejipanga kuhakikisha wanalipa kisasi.Kocha wa timu hiyo, Abdel ben Kacem, amesema amewajua vizuri Yanga na kwa maandalizi waliyoyafanya anaamini atafanikiwa kulipa kisasi. Katika hatua nyingine, kocha wa Simba, Jackson Mayanja, ameitabiria ushindi Yanga katika pambano la leo kwani wapinzani wao ni timu ambayo haina jina kubwa katika soka.“Sitaki kuizungumzia sana Yanga, lakini nawapa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo, kwa sababu wana timu nzuri na tayari wana akiba ya bao kufuatia ushindi walioupata ugenini, lakini hata timu wanayocheza nayo ni dhaifu,” alisema Mayanja.
4
TIMU ya taifa ya riadha itakayoshiriki mashindano ya 17 ya dunia inatarajia kuagwa jijini Arusha Septemba 23, imeelezwa. Tanzania katika mashindano hayo ya Dunia yatakayofanyika Qatar mwaka huu kuanzia Septemba 27 hadi Oktoba 6, itapeleka wanariadha wanne tu, watatu wakiume na mmoja wakike, wote wakishiriki mbio za marathoni.Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday alisema jana kuwa, timu hiyo ambayo itakuwa na wanariadha wanne na viongozi watatu wa RT, itaagwa jijini Arusha tayari kwa safari siku inayofuata. Wanariadha hao na muda wao bora katika mabano ni Augustino Sulle (2:07:44), Alphonce Simbu (2:08:27) na Stephano Huche (2:12:24) wakati mwanamke pekee katika msafara huo ni Failuna Abdi (2:27:36).Gidabuday alisema mwanariadha mwingine aliyefuzu kushiriki mashindano hayo ya dunia ni Ezekiel Ngimba 2:13:34, lakini kutokana na kanuni za Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Riadha (IAAF) kuruhusu nchi kuwa na wachezaji watatu katika mchezo mmoja, Ngimba ameenguliwa sababu ya muda wake kutokuwa mzuri. Gidabuday alisema kuwa hivi karibuni watamtangaza mgeni rasmi atakayekabidhi bendera timu hiyo, ambayo watu wengine wanaotarajia kuwemo ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa RT, William Kallaghe, ambaye anamuwakilisha Rais wa shirikisho hilo, Antony Mtaka. Wengine wanaotarajia kuwemo katika msafara huo ni Gidabuday mwenyewe na makamu wa pili wa RT, Dk Hamad Ndee. Timu hiyo kwa mujibu wa Gidabuday, itaondoka mafungu mawili, ambapo kundi la kwanza, ambalo litakuwa na Kallaghe na Failuna wataondoka mara baada ya kuagwa wakati fungu jingine litaondoka Oktoba 2. Alisema Failuna anawahi kwa kuwa mbio yake itachezwa siku ya ufunguzi wa mashindano hayo Septemba 27 wakati Kallaghe anawahi sababu ya Mkutano Mkuu wa IAAF, ambao utakuwa pia na Uchaguzi Mkuu.Mkutano Mkuu wa 52 wa uchaguzi utafanyika Septemba 25 na 26 na utawachagua Rais wa IAAF, makamu wanne wa rais na wajumbe 13 wa Kamati ya Utendaji.
4
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Mohammed Dewji ametembelea Uwanja mpya wa mazoezi wa timu hiyo na kufafanua kuwa kwa hatua nzuri ya ujenzi iliyofi kiwa, utaanza kutimika rasmi mwishoni mwa mwezi ujao. Oktoba 24 mwaka jana, kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram alionyesha sehemu ya ujenzi ambapo wahandishi walionekana kuendelea na ujenzi ambapo alisema uwanja huo utatumika hata baada ya kutoweka duniani. Mo Dewji alisema alitembelea viwanja viwili, ambapo kwa pamoja vitaanza kutumika mwezi hivi karibuni ambapo kupitia picha alizoonesha kwenye mtandao wake huo viwanja hivyo vilionekana kuwa tayari na nyasi za bandia. Alisema viwanja hivyo vitafunguliwa sambamba na vyumba vya kubadilishia nguo na kuongeza kuwa anatarajia kuona timu yake ikifanya mazoezi kwenye viwanja hivyo kuanzia mwishoni mwa mwezi wa kumi mwaka huu. Kwa muda miaka mingi klabu ya Simba imekuwa ikipambana kujenga uwanja wao wa mazoezi bila mafanikio ila ujio wa mwekezaji Mo Dewji ni wazi umelahisisha baadhi ya mambo muhimu kukamilika.
4
PRETORIA, AFRIKA KUSINI TAASISI ya kupamba na rushwa  ya Afrika Kusini imesema Rais Cyril Ramaphosa alisema uongo juu ya kiasi cha rand 500,000 ($35,900) takribani shilingi za kitanzania  milioni 83 kilichochangwa na yeye kupokea kwa ajili ya kampeni zake za kuongoza chama cha African National Congress (ANC). Ramaphosa, ambaye alichukua nafasi ya Rais wa zamani Jacob Zuma mwaka jana na baadae kushinda uchaguzi wa urais na hata  kuapa kupambana na rushwa, alikana kufahamu juu ya mchango huo wakati alipoulizwa na Bunge mwezi Novemba. Awali Ramaphosa aliwaambia wabunge kuwa malipo hayo yalikuwa ni kwa ajili ya mwanae wa kiume, Andile ambaye alilipwa kwa kazi ya ushauri alioutoa kwenye kampuni ya Bosasa, ambayo sasa inafahamika kama African Global Operations. Baadae alikiri kuwa mchango huo ulikuwa ni kwa ajili ya kampeni zake za kuwa kiongozi wa ANC. Mkuu wa Taasisi hiyo ya Kupambana na Rushwa,  Busisiwe Mkhwebane, ambaye anachunguza tuhuma zinazodaiwa kufanywa na viongozi wa serikali, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Ramaphosa alikuwa amevunja Katiba  na kanuni za utendaji wa maadili katika jibu lake hilo kwa Bunge. Katika ripoti iliyotolewa jana, Mkhwebane  alisema; ” Ingawa Rais Ramaphosa anaweza kuwa na haki ya kurekebisha taarifa ya awali kwa taarifa yenye kosa au ambayo haijakamilika, lakini alipotosha Bunge, “. Alisema Rais alitakiwa kujipa muda yeye mwenyewe kuchunguza kwa ajili ya kutoa majibu sahihi kabla ya kujibu swali kutoka kwa kiongozi wa Chama Kikuu cha Upinzani cha Democratic Alliance, Mmusi Maimane. “Kwa hiyo nimebaini kuwa kitendo cha Ramaphosa …ingawa kinaonekana ni cha nia njema, lakini ni kinyume na ofisi yake “. Pia ripoti hiyo imebaini kuwa njia ambayo michango hiyo ilipita kwenye akaunti mbalimbali ikiwamo ile ya kampeni ya Ramaphosa, imeacha shaka ya kuwapo kwa fedha chafu. Tayari Mkhwebane amewasilisha ripoti hiyo kwenye Kamati ya Bunge ya Maadili, ambayo huenda ikachunguza zaidi. “Watakachobaini ndicho kitakachoonyesha njia ya nini kitatokea baada ya hapo, lakini hii bado haiwazuii wabunge kupeleka hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani naye kwa spika,”  aliongeza.  “Si kwamba hicho ndicho kitatokea lakini inaweza kuwa njia mojawapo kwa sasa.” Alisema ZUMA AGOMA KUHOJIWA TENA Wakati huo huo  Wakili wa rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ameiambia tume inayochunguza madai ya ufisadi dhidi ya kiongozi huyo kwamba mteja wake hataweza kushiriki tena mahojiano na tume hiyo kwa sababu anaamini kuwa hatendewi haki kwenye mahojiano hayo. Wakili huyo  Muzi Sikhakhane aliiambia tume hiyo ya uchunguzi jana kuwa  hawataendelea kushiriki vikao vya uchunguzi, kwani Zuma amekuwa muhanga wa maswali ya kuchafua na kuudhi. Zuma alikuwa anatarajiwa kufika katika tume hiyo jana kwa ajili ya kuendelea na mahojiano hayo, akiwa tayari ameshahudhuria mengine katika siku tatu zilizopita na  kutoa ushahidi, kabla ya mawakili wake kuomba kuahirishwa kwa mahojiano hayo. Uchunguzi huo, ambao Zuma alikubali kuunda katika wiki za mwisho za utawala wake, unaangazia madai ya ufisadi pamoja na matumizi ya ushawishi ambayo yalikuwapo katika utawala wake wote wa miaka tisa madarakani. Mapema wiki hii baada ya kuonekana kwa mara ya kwanza mbele ya timu inayochunguza tuhuma hizo Zuma alimwambia jaji anayeongoza uchunguzi  huo kwamba tuhuma hizo zilikuwa ni njama za kumwondoa kwenye ulingo wa siasa. Zaidi alizishutumu taasisi za kiusalama za kigeni, ambazo hakuzitaja  kuwa zilikuwa nyuma ya mpango huo uliosukwa kwa miongo kumwondoa madarakani. Tuhuma dhidi ya Zuma ni zile zinazolenga uhusiano wake wa shaka na familia ya Gupta ambayo inashutumiwa kushawishi uteuzi wa baraza la mawaziri na zaidi kushinda tenda zenye faida kubwa kwa njia ya rushwa katika serikali yake. Pia alikuwa anatuhumiwa kuchukua rushwa kutoka kampuni ya Bosasa, inayoendeshwa na familia ya Watson. Hata hivyo Zuma alipinga tuhuma kwamba aliruhusu serikali ishikwe na familia ya Gupta, au kuuza nchi.
2
Hatua hiyo pia imesababisha idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa pia kushuka kwa asilimia 84 hadi kufikia Sh milioni 1.8 kutoka milioni 11.6. Akizungumza jana kuhusu taarifa ya soko katika mauzo yaliyofanyika wiki iliyopita, Meneja Miradi na Biashara wa DSE, Patrick Mususa alitaja kampuni tatu zilizoongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa kuwa ni Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) asilimia 39.72, benki ya CRDB asilimia 26.18 na Kampuni ya Saruji Tanga (TCCL) asilimia 24.39.Mususa alisema idadi ya mtaji wa soko la hisa la Dar es Salaam imeshuka pia kutoka Sh trilioni 21 hadi Sh trilioni 20.2 katika mnada wa mauzo ya hisa uliofanyika wiki hii. Alisema idadi ya mtaji wa kampuni ya ndani pia imeshuka kutoka Sh trilioni 9.8 hadi kufikia Sh trilioni 9.6.Akizungumzia mabadiliko ya bei za hisa, alisema kampuni moja imejitokeza kuongoza katika ongezeko la bei ya hisa wiki iliyopita ambayo ni kampuni ya Nation Media (NMD) kwa asilimia 7.14.Kwa upande wa viashiria vya sekta, Mususa alisema kiashiria cha sekta ya viwanda kimeshuka kwa pointi 9.3 kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa kwenye kaunta za Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kwa asilimia 0.62 na TCCL kwa asilimia 0.37.
5
POLISI mkoani Morogoro inamshikilia Keneth Mwangele (69), mkazi wa kijiji cha Kiegea, Wilaya ya Kilosa na kumsaka mwanamke anayetambuliwa kwa majina ya Zaida Kaita Manjoge Rose akituhumiwa kuiba mtoto mwenye umri wa miezi saba aitwaye Jackson John.Mtoto huyo aliibwa maeneo ya Stendi Kuu ya Mabasi ya Msamvu, Manispaa ya Morogoro kwenye mazingira tatanishi alipokuwa na mama yake Raheli Stanfod (21), mkazi wa Berega, wilayani Kilosa.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkakati wa jeshi hilo kuzuia na kupambana na uhalifu na wahalifu.Amesema tukio hilo lilitokea Agosti 7, mwaka huu saa tano asubuhi maeneo ya Stendi Kuu ya Mabasi Msamvu, Manispaa ya Morogoro ambapo Raheli aliibiwa mtoto wake Jackson.Akizungumzia mazingira ya wizi wa mtoto huyo amesema, mwizi wa mtoto alikwenda katika kijiji cha Kiegea , Kata ya Berega kwa lengo la kutafuta msichana wa kazi za ndani ndipo alipokutana na mzee aitwaye Keneth Mwangele (69) mkazi wa kijiji hicho na yeye alimpeleka nyumbani kwa kina Raheli baada ya kumweleza lengo lake la kufika kijijiji hapo.Amesema, baada kufika nyumbani hapo walionana na mmiliki wa mji huo yaani baba yake Raheli mzee Stanfod Chabonga (64), ndipo alipomtambulisha ujio wa mgeni huyo na kumtoa hofu kwamba anatafuta binti wa kwenda kumsaidia kazi jijini Dar es Salaam.Kamanda huyo wa Polisi alisema mara baada ya kujiridhisha mzee Chabonga aliamua kuwakutanisha na Raheli kwa lengo la kuzungumza ili wakikubaliana aende akafanye kazi mkoani Dar es Salaam kwa maana mgeni huyo alihitaji msichana hata kama ana mtoto mdogo.Amesema hata hivyo wakiwa safarini kuelekea Dar es Salaam walipofika Stendi Kuu ya Mabasi Msamvu wakati wanasubiri gari ya kwenda Dar es Salaam ndipo mwizi huyo alipopata nafasi ya kumchukua mtoto kutoka kwa mama yake akijifanya anamsaidia na kwenda kutafuta chakula ndipo alipotokomea kusikojulikana.Amesema hadi sasa mtuhumiwa anashikiliwa ambaye ni mzee Mwangele aliyempeleka mwizi huyo nyumbani kwa mama mtoto na jitihada za kumtafuta mwizi huyo bado zinaendelea.Kutokana na sakata hilo alitumia fursa hiyo kuwasihi wazazi na walezi wenye watoto kutowaamini watu wasiowafahamu kuwaachia watoto kwani baadhi yao hawana nia nzuri .
3
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya wa Kisarawe Mussa Gama amesema, kufunguliwa jengo la kisasa la abiria kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam ni fursa kubwa ya uchumi kwa wilaya hiyo.Amesema, kufunguliwa kwa jengo hilo kutaongeza idadi ya watalii wanaoutumia hivyo ni fursa ya kujenga hoteli za kisasa kwa kuzingatia ukaribu na urahisi wa kutoka Kisarawe kwenda JNIA.Kwa mujibu wa Gama JNIA upo umbali wa km 18 kutoka mjini Kisarawe na mtu anaweza akatumia takribani dakika 10 kutoka mjini hapo hadi uwanjani.“Ukiangalia hoteli nyingi zimekaa upande wa Dar es Salaam na Dar es Salaam sasa hivi wanaweza wakawa wanachelewa sana kwenda katika uwanja wa ndege lakini ukitokea Kisarawe kwenda uwanja wa ndege ni kilometa chache tu kwa hiyo kun fursa hiyo ya uwekezaji wa hoteli za kisasa” amesema Gama.Amesema, Kisarawe ni eneo sahihi la kujenga hoteli kwa kuwa kuna maeneo kwa ajili ya utalii wa haraka haraka wa siku moja au siku chache wakati mgeni anasubiri siku ya kusafiri kwa kutumia JNIA.Ametoa mfano kuwa, mgeni anaweza akashuka JNIA, akafikia kwenye hoteli iliyopo Kisarawe, akaenda kutalii Kisarawe kwa siku moja na kurudi uwanjanni hapo kuendelea na safari.Gama amesema, misitu ya Pugu na Kazimzumbwi inatumika kwa utalii wa picha, na utalii wa upandaji milima.
5
  Na MWANDISHI WETU, Sumbawanga WAJAWAZITO wanaokwenda kujifungua katika zahanati ya Kijiji cha Chipu, Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, wanalazimika kubeba ndoo za maji kichwani na vibatari kwa vile zahanati hiyo haina umeme. Mganga Mkuu wa zahanati hiyo, Gasper Kachinga, alisema hayo juzi wakati akipokea msaada wa vitanda viwili vya kujifungulia vilivyotolewa na Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Aeshi Hilaly, ambavyo thamani yake ni Sh milioni 2.5. Kutokana na kukosekana kwa huduma za maji na umeme katika zahanati hiyo, wagonjwa huagizwa  kwenda na vibatari na ndoo za maji waweze kupata huduma. Zahanati hiyo ilikuwa na kitanda kimoja cha kujifungulia wakati wagonjwa wengine hulala sakafuni au kupeana zamu. Hilaly alisema kijiji hicho ni miongoni mwa vijiji vitakavyonufaika na mradi wa maji wenye thamani ya Sh bilioni 2.1 na kwamba mkandarasi tayari amepatikana na yupo katika hatua za awali za kuanza utekelezaji. Akizungumzia ukosefu wa umeme, mbunge huyo alisema kero hiyo itakwisha katika muda mfupi kuanzia sasa  kwa vile Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) limeanza mchakato wa kufikisha umeme kijijini hapo. Alisema wakati huduma ya umeme ikisubiriwa, atanunua taa maalumu ambazo zitatumika katika zahanati hiyo kuwasaidia kina mama hao wasiendelee kujifungua kwa vibatari. Hilaly aliushauri uongozi wa kijiji hicho kuweka utamaduni wa kuvuna maji ya mvua, hasa wakati wa kipindi hiki cha masika kupunguza uhaba wa maji.
3
NA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM UONGOZI wa klabu ya Azam FC, umetamba kurejea kileleni kwa kishindo kwa kuziombea njaa timu za Simba na Yanga zipoteze kwenye michezo iliyobakia ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Azam ipo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu, baada ya kucheza michezo 19 na kufanikiwa kufikisha pointi 42, Jumamosi hii inatarajia kucheza mchezo wake wa 17 ugenini dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Wakati timu hiyo ikijiandaa kukabiliana na Mbeya City, vinara wa ligi hiyo Simba na Yanga watakuwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kukamilisha mchezo wa 20 kwa Simba na Yanga wa 19 ambao utakuwa muhimu kwa kila timu ili kupata nafasi ya kuongoza. Akizungumza na MTANZANIA, Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Saad Kawemba, alisema mchezo dhidi ya Mbeya City utawafanya kurudi kwenye mstari baada ya kupata kichapo cha bao 1-0 dhidi ya timu ya Coastal Union. “Adui yako muombee njaa, huo ndio utaratibu wa ligi, unapopoteza mwingine anachukua nafasi,” alisema Kawemba. Kawemba alisema japokuwa rekodi yao ya kutofungwa michezo 18 imevurugwa na Coastal Union, wamejipanga kuhakikisha wanapambana ili kurejea  nafasi ya juu ya msimamo wa ligi hiyo. “Tutarudi kwenye rekodi yetu ya ugenini muda si mrefu, wabaya wetu ambao wanasubiri tufungwe ndio wazungumze watasubiri sana,” alisema Kawemba.
4
MKUTANO wa 14 wa Bunge la 11 unatarajia kuanza leo jijini Dodoma, ambapo Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa wa Mwaka 2018 ni kati ya miswada mitano, itakayojadiliwa na kupitishwa na Bunge.Aidha, Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea (CCM) anatarajia kula kiapo cha uaminifu. Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa ya Ofisi ya Bunge, kuhusu ratiba ya shughuli za Bunge zitakazofikia tamati yake Februari 8 mwaka huu, inaonesha kuwa miswada mitano itajadiliwa na kupitishwa.Miswada mingine itakayojadiliwa ni Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania wa mwaka 2018, Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini wa mwaka 2018, Muswada wa Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa mazingira wa mwaka 2018, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 4 wa mwaka 2018.“ Katika Mkutano huu wa Kumi na Nne, wastani wa maswali 125 ya Kawaida yanatarajiwa kuulizwa na Wabunge. Aidha, wastani wa maswali 16 ya papo kwa papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yanatarajiwa kuulizwa kwa siku za Alhamisi ya Januari 31, na Januari 7, 2019,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.Aidha, katika mkutano huo pia Kamati za Kudumu za Bunge 15, zitawasilisha taarifa za mwaka za kazi za Kamati hizo kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 117(15) ya Kanuni za Bunge.Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma, Kamati ya Bajeti, Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Kamati ya Miundombinu.
3
HALMASHAURI ya wilaya ya Chamwino imetenga eneo la uwekezaji katika kijiji cha Dabalo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha sukari kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha tani 15,000 kwa mwaka kitakapokamilika. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Athumani Masasi. Alisema hayo wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za serikali za halmashauri hiyo katika mkutano wa mwaka wa baraza la madiwani kwa kipindi cha Julai mwaka jana hadi Juni mwaka huu kilichofanyika jana.Alisema eneo hilo la uwekezaji lina mashamba mengi ya miwa, imefanikiwa kumpata mwekezaji Purandare Industries Tanzania LTD kutoka India kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha sukari. Kiwanda hicho kitakapokamilika kitakuwa na uwezo wa kutoa ajira kwa Watanzania wasiopungua 2,000 na kitaongeza idadi ya wakulima watakaozalisha miwa zaidi ya 3,000. Aidha halmashauri hiyo itajenga kiwanda cha kusindika zabibu kitakachojengwa eneo la Chinangali B na cha maembe kitakachojengwa katika kijiji cha Huzi ndani ya wilaya hiyo ya Chamwino.Alisema halmashauri hiyo imejipanga kujitegemea katika kujiendesha kwa kutumia mapato yake ya ndani kwa kiwango cha asilimia 65 ifikapo mwaka 2022, ikilinganishwa na asilimia tano ya mwaka huu. Pia alisema halmashauri hiyo imefanikiwa kupokea Sh milioni 900 kwa ajili ya ukarabati na kujenga miundombinu ya vituo vya afya vya Chamwino na Mpwayungu.
3
KUCHA na kope za bandia wanazobandika wanawake zimewagawa wabunge, hata hivyo wengi wao wamesema kubandika huko ni kumfundisha Mungu namna ya kuumba na kukosoa uumbaji wake. Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma jana, wabunge wengi bila kujali itikadi za vyama vyao walisema, wanawake wanatakiwa kuheshimu uumbaji wa Mungu na kuacha kukosoa uumbaji wake.Mbunge wa Viti Maalumu, Zainabu Vullu (CCM) alisema kuweka kope na kucha za bandia ni kumfundisha Mungu namna ya kuumba binadamu. “Kucha, kope pamoja na mavazi yanatakiwa kuwa yale yanayompa heshima Mbunge,” alisema. Alisema wanawake wanajichubua na kupaka mikorogo, kiimani wanajiharibia miili na afya yao, waliotengeneza wanataka kuleta athari kwa binadamu wenzao. Vullu alisema wabunge ni kioo cha jamii, chochote kinachofanywa nao kinaigwa na jamii, hivyo matendo na tabia zao zinatakiwa kuwa za mfano kwa jamii ili kuiga.“Mbunge ni kioo anatakiwa kuwa katika hali nadhifu ili jamii ijifunze kutokana na mwonekano na uwepo wake, kwa kuweka kope za bandia na kucha ataelekezaje jamii?” alihoji. Mbunge Vullu alisema, kuhusu Spika Job Ndugai kutamka hivyo, ni haki yake na kwa mamlaka yake anaweza kukemea chochote na yeye anaunga mkono tamko hilo la kupiga marufuku kuweka kope na kucha za bandia. Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (Chadema), alisema kanuni za Bunge zinasema kuhusu mavazi, wala hazisemi lolote kuhusu kucha na kope za macho za kubandika.Alisema kupaka kucha bandia na kope ni uhuru wa mtu na wala Bunge halitaweza kudhibiti watu wanaoingia wakiwa wameweka kope na kucha za bandia. Mbunge wa Mbinga Vijijini (CCM), Martin Msuha alisema Spika alikuwa na haki ya kupiga marufuku kucha na kope za kubandika, akasema walipokuwa Zanzibar kwenye mkutano wa maadili, aliombwa aangalie mavazi ya wabunge wakati wanapokuwa kwenye kamati mbalimbali za Bunge. “Spika aliwataka wenyeviti wa kamati kuangalia mavazi ya wabunge wanapokuwa kwenye kamati yanatakiwa kuwa ya heshima,” alisema.Alisema Spika hajakosea ni haki yake kwani Mbunge ni mtu anayetakiwa kuonekana mfano bora kwa jamii, hivyo kuweka kucha za bandia na kope za bandia ni kutokuwa na maadili. Mbunge wa Viti Maalumu, Alfredina Kaigi (CUF) alisema Mungu aliwaumba viumbe wake wote wakawa wazuri, kitendo cha kuweka kucha na kope za bandia ni kukosoa uumbaji wa Mungu. Alisema mbunge ni kioo cha jamii, hivyo kitendo cha kujichubua ni aibu kwani unakuwa unaharibu ngozi ya asili ambayo inatambulisha Uafrika. Kaigi alisema kitendo cha Spika Ndugai kupiga marufuku hajakosea, kwani wabunge wanatakiwa kuonekana mfano wa kuigwa na jamii, badala ya kuharibu ngozi yao.Mbunge wa Hanang, Dk Mary Nagu (CCM) alisema; “Kwa nini kubandika kucha na kupe wakati Mungu alikuumba vizuri. Kitendo cha kujichubua wakati ngozi ya asili ni njema inaonekana unataka kurekebisha uumbaji wa Mungu. “Wanawake wanatakiwa kutunza ngozi ya asili ambayo inatambulisha Uafrika wake, kwani ngozi ya asili ni nzuri na inatakiwa kutunzwa badala ya kuichubua,” alisema. Hata hivyo, Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya (Chadema) alisema kope na kucha pamoja na kupaka wanja siku hizi vitu hivyo vinafanyika kitaaluma zaidi kwa kupaka unga katika kucha na zinakuwa ngumu, hivyo kitendo cha kuwakata kubandika ni udhalilishaji wanawake.“Spika alitakiwa pia kuzungumza kuhusu wabunge wanaume ambao wamekuwa wakivuta sigara kupita kiasi pamoja na kulewa, kwani nao wanakuwa wamekosea,” alisema. Mbunge wa Kilwa Kusini, Vedasto Ngombale (CUF) alisema; “Kubandika kope na kucha kunakiuka utamaduni wetu, ni mapambo yaliyopitiliza kuliko mapambo ya kawaida ambayo mwanamke anaweza kujipamba.” Mbunge wa Viti Maalumu, Joyce Sokombi (Chadema), alisema wabunge wanatakiwa kujitambua kwani ni viongozi wa mfano, hivyo wanatakiwa kufuata maadili ya Bunge na kuachana na kitendo cha kumkosoa Mungu katika uumbaji wake.
3
TANZANIA ni nchi ya 12 katika uzalishaji muhogo duniani na ya sita barani Afrika baada ya Nigeria, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Ghana, Angola na Msumbiji.Akifungua mkutano ya siku tatu wa wadau wa sekta ya muhogo wakiwemo watunga sera, watafiti, sekta binafsi na wakulima waliokutana jijini hapa, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Profesa Siza Tumbo alisema muhogo ni zao la pili kwa umuhimu likitanguliwa na mahindi.Profesa Tumbo alisema uzalishaji wa muhogo nchini, kila mwaka unachangia asilimia 5.5. ya uzalishaji wa muhogo duniani na asilimia 14 ya uzalishaji Afrika. Profesa huyo alisema mahitaji ya baadaye ya muhogo nchini, yataongeza uzalishaji na kuwa kati ya tani 530,000 na 630,000, hali hiyo inachangiwa na kuongeza thamani ya muhogo.“Thamani ya muhogo inaongezeka kutokana na kutengeneza unga, wanga na kuwa malighafi katika viwanda vya bia, pipi na vitafunio, viwanda vya nguo, karatasi na mbaongumu, rangi na dawa,” alisema.Mkutano huo umeandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), Taasisi ya Kimataifa ya Kitropiki (IITA) na Wizara ya Kilimo, Kitengo cha Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP), unalenga kuhimiza wadau kuongeza uzalishaji zao hilo.Alisema asilimia 84 ya uzalishaji nchini ni kwa matumizi ya chakula cha binadamu, lakini uzalishaji wake bado upo chini na zao hili halijatumika kikamifu. “Ninawahimiza washiriki kuendeleza hatua ya kukubiliana na changamoto ambazo zimekuwa zikikabili jitihada za kufanya muhogo kuwa zao la biashara ili kuboresha mapato ya wakulima wadogo na kusaidia nchi yetu kuelekea kufikia Dira ya Maendeleo ya 2025,” alisema.
3
Na Mwandishi Wetu -DODOMA NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Angeline Mabula, ameagiza kupitiwa upya mkataba wa mauziano ya nyumba 4,000 kati ya Kampuni ya PMM 2001 Ltd na wakazi wa Vingunguti, Dar es Salaam. Uamuzi huo unafuatia kutozingatiwa kwa masharti ya mkataba ulioingiwa awali, ambao umeonekana kuwa na upungufu wa kisheria na hivyo kusababisha PMM 2001 Ltd kushindwa kuwalipa wamiliki wa nyumba katika eneo la Vingunguti kwa karibu miezi tisa kama walivyokubaliana jambo lililozua taharuki. Dk. Mabula alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki, baada ya kukutana na pande zote mbili za kamati inayosimamia makubaliano ya uuzaji nyumba 4,000 katika mitaa minne ya Vingunguti ambayo ni Mnyamani, Mtambani, Mtakuja na Faru, Kampuni ya PMM 2001 Ltd na Mbunge wa Segerea, Bonnah Kamoli katika ofisi za wizara hiyo, jijini hapa. Alisema baada ya kupitia mkataba wa mauziano ya nyumba katika eneo la Vingunguti, kati ya PMM 2001 Ltd na wamiliki wa nyumba, wamebaini kutofuata taratibu za kisheria na kubainisha kuwa wamiliki ambao hawajalipwa fedha yoyote hawabanwi na mkataba huo na wanaweza kuzifanyia shughuli yoyote nyumba zao. “Kwa zile nyumba 80 ambazo PMM 2001 Ltd ilizinunua kwa wamiliki katika eneo hilo, wizara itatuma timu maalumu kufuatilia iwapo kampuni hiyo imefuata taratibu zote za mauziano, ikiwamo kutoa kodi ya Serikali,” alisema. Kuhusu suala la wamiliki wa nyumba 17 ambao kampuni hiyo imewalipa Sh milioni 35 kwa kila mmoja kama fedha za awali, aliagiza hatua za kisheria zifuate kwa kuwa mkataba wa mauziano hauoneshi kiasi kilichobaki. Dk. Mabula alisema kilichofanywa na PMM 2001 Ltd kwa wamiliki, ni udanganyifu unaoweza kutoa mwanya mkubwa kupoteza haki yao na kusisitiza Serikali  haiko tayari kuona  wananchi  wanapata tabu kufuatilia haki zao.  Alisema atamwagiza Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Dar es Salaam kuzungumza na wananchi wanaouza nyumba kwa kampuni hiyo. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Fedha na Utumishi wa PMM 2001 Ltd, Damian Kanuti, alijitetea kwa kueleza  kampuni yake ilishindwa kutekeleza makubaliano ya ununuzi wa nyumba katika mitaa ya Vingunguti kutokana na kuchelewa kupata mkopo ilioutarajia kutoka Benki ya TIB na kubainisha kuwa pamoja na sakata hilo, walishalipa Sh bilioni 1.7, ikiwa ni malipo ya nyumba 80 na fedha ya awali kwa wamiliki 17. Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamia Uuzaji Nyumba 4,000 katika eneo la Vingunguti, Ramadhani Pepo, aliilalamikia kampuni  hiyo kwa kutoonesha ushirikiano kwa kamati wakati wa mauziano.
3
Katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi jana Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Chamwino, Aithan Chaula alisema ekari 300 nyingine zimeongezwa ambapo wananchi wanaoishi vijiji karibu na shamba hilo wamegawiwa ekari moja kila moja ambapo sasa wameanza kusafisha na kuchimba mitaro.Sasa shamba litakuwa la ekari 600.“Kama tutakwenda sawa sawa mwisho wa mwaka huu shamba lote litakuwa limepandwa,” alisema.Alisema wananchi waliopata maeneo hayo wanachimba mitaro kwa nguvu zao kwani waliona mafanikio waliyopata wenzao 300 wa kwanza wanaolima zabibu katika eneo hilo.Alivitaja vijiji ambavyo wananchi wake wamepatiwa maeneo kwa ajili ya kulima zabibu kuwa ni Chinangali 2, Manchali, Makoja, Buigiri, Mlebe na Chamwino.Alisema wakulima wa kwanza 300 ni wanachana wa Fune Saccos na Chabruma Amcos ambao wamekuwa wakipata mikopo kwenye taasisi za kifedha, hali ambayo iliwavutia wananchi wengi zaidi na kuona faida za kilimo cha zabibu.Alisema shamba hilo lina miundombinu ya umwagiliaji kwa kutumia matone na ni moja ya mashamba makubwa ya zabibu katika mkoa wa Dodoma.Pia alisema kuna shamba jipya la zabibu Mvumi Makulu ambapo kuna ekari 323 na wananchi watachimba mitaro kwa nguvu zao huku wakisaidiwa na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP).Chaula alisema lengo la kuwa na mashamba makubwa kwenye eneo moja kunarahisisha upatikanaji wa huduma za ugani, miundombinu ya maji, umwagiliaji, upatikanaji wa mikopo na kwenda pamoja katika kuongeza thamani ya zao husika.
5
Samba iliyowasili Zanzibar Jumapili iliyopita ipo mjini hapa na wachezaji 18 ambao wote wapo katika afya njema, ambao wanajifua kwa ajili ya mechi hizo pamoja na ile dhidi ya Azam FC itakayofanyika Desemba 12.Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mratibu wa Simba, Abass Suleiman alisema kuwa ratiba ya mazoezi yao itakuwa ikibadilika badilika, ambapo siku nyingine watakuwa wakifanya mazoezi asubuhi na jioni.Alisema kuwa siku nyingine watakuwa wakifanyia mazoezi katika ufukweni wakati wa asubuhi na jioni kwenye Uwanja wa Amaan, lalini watakuwa wakibadili ratiba kulingana na mazingira.Hata hivyo, alisema kuwa mazoezi ambayo wanyafanya si kwa ajili ya mechi moja tu ya Azam bali wanafanya kwa ajili ya mechi zote ambazo zinawakabili katika Ligi Kuu Tanzania Bara.Alisema maandalizi hao mbali na Azam, pia Desemba 19 wanatarajia kucheza na Toto African jijini Mwanza na Desemba 26 watakwaana na Mwadui ya Shinyanga. Simba wapo Zanzibar kwa ajili ya kambi ya wiki moja na wanatarajia kuondoka Desemba 10 tayari kwa mchezo wao dhidi ya Azam FC jijini Dar es Salaam.
4
NA MWANDISHI WETU KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameitaka Serikali itangaze rasmi baa la njaa kwa mujibu wa sheria. Zitto alitoa kauli hiyo jana katika mkutano wa hadhara wa kumnadi mgombea udiwani wa Kata ya Nkome mkoani Geita kupitia ACT-Wazalendo. “Hali ya chakula nchini si nzuri. Wananchi mmeshuhudia namna bei za vyakula zinavyopanda kila siku. Bei ya sembe sasa kilo moja imefikia shilingi 1,600 pale Morogoro, kilo moja ya mchele ni shilingi 1,500, maana yake leo ugali na wali imekuwa bei inafanana. Gharama za maisha zitaendelea kupanda kutokana na uhaba wa chakula kuwa mkubwa. “Kwanini hali ya chakula inazidi kuwa mbaya? Ni kwa sababu ya uamuzi mbovu wa Serikali kuhusu hifadhi ya chakula. Serikali zote zilizopita huko nyuma zilikuwa zinanunua chakula cha akiba ili wakati wa ukame kama sasa chakula hicho kiingie sokoni na hivyo kushusha bei na kuwezesha wananchi kumudu gharama za chakula. “Rais wetu kawaambia wananchi wa Kagera kwamba Serikali haina shamba hivyo hakuna chakula cha njaa. Hii kauli si ya uongozi. Ni kauli ya kuficha uamuzi wa Serikali uliotusababisha kukosa akiba ya chakula,” alisema. Zitto alisema Ghala la Taifa la Chakula (NFRA) lina tani 90,000 tu za chakula wakati kwa kipindi kama hiki mwaka juzi lilikuwa na tani 450,000. Kwa mantiki hiyo, alisema chakula kilichopo kwa sasa ndani ya ghala hilo kinatosha kwa wiki moja kwa mujibu wa takwimu katika taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa mapitio ya uchumi ya Novemba, mwaka jana. “Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dk. Charles Tizeba, alijibu hoja hizi kwa wepesi kabisa na kusema kwamba Tanzania ina chakula cha kutosha. Alipoulizwa ataje kiasi kilichopo NFRA, alijibu kwa sababu za kiusalama hawezi kutaja,” alisema. Zitto alikwenda mbali kwa kumpongeza  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kwa kuamua yeye mwenyewe kutembelea NFRA na kujionea hali halisi. Alisema alichokifanya Majaliwa ndio uongozi na si viongozi kukanusha habari ambazo ni za kweli na zilishathibitishwa na taasisi za Serikali kama BoT na alimtaka kuwachukulia hatua viongozi wa Serikali wanaoficha ukweli kuhusu baa la njaa. “Waziri wa Kilimo anasema kama wananchi wanaona ugali ni ghali wale wali. Anasema kuna mchele mwingi nchini, lakini umeshikwa na watu binafsi. Waziri anataka kuwaambia Watanzania kuwa hivi sasa Serikali inategemea chakula cha watu binafsi ambao haijui idadi ya tani zilizopo kushughulika na suala la njaa. “Hii ni ajabu kubwa sana, nchini Ufaransa alitokea mke wa mfalme mmoja. Wananchi walikuwa wanalalamika kuwa hakuna mikate. Malkia yule akiitwa Marie Antonnoite, alimwambia mumewe, hawa watu wako kama hawana mikate si wale keki? Hii ndio hali ya sasa nchini. Waziri anasema kama sembe imekuwa ghali, wananchi wale wali. Anasahau kuwa hata mchele umepanda bei. Maharage yamepanda bei na mafuta ya kupikia yamepanda bei,” alisema.  Kauli ya Majaliwa Katikati ya wiki hii, Majaliwa, akiwa mkoani Ruvuma alitoa agizo la kusisitiza kutunza chakula kwa kusema akiba ya mahindi iliyopo iendelee kutunzwa hadi msimu ujao wa mavuno. Alitoa agizo hilo baada ya kukagua maghala ya nafaka yanayomilikiwa na NFRA Kanda ya Songea. Alisema kawaida mwezi huu mvua za kutosha huwa zinanyesha na huwa kuna baridi lakini mwaka huu imekuwa tofauti kwa sababu kunashuhudia kuwapo joto kali. “Kama mvua haijanyesha hadi leo ni lazima tuchukue tahadhari, hata mvua ikija hatujui itaendelea kunyesha hadi lini na kwa kiasi gani,” alisema. Majaliwa aliwataka wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi wa halmashauri kutoa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji wa akiba ya chakula.
3
Taifa Queens wakati wa kuanza mashindano hayo Jumapili iliyopita, ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri kutokana na kuwa juu kiviwango vya mchezo huo duniani, ukilinganisha na timu zingine shiriki.Tanzania ni ya 15 kwa viwango vya ubora kwa mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Netiboli (INF), huku ikifuatiwa na wenyeji Botswana ambao wako katika nafasi ya 16, Zambia (18), Zimbabwe (26), Namibia (31) na Swaziland (33).Kwa mujibu wa toleo la jana la gazeti la Herald la Zimbabwe, timu ya taifa ya Zimbabwe ilitwaa taji hilo la Afrika baada ya kushinda mchezo wa mwisho kwa mabao 37-28 dhidi ya Taifa Queens.Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, washindi walikuwa mbele kwa mabao 19-14 huku robo ya tatu, Zimbabwe ilikuwa mbele kwa 30-18 na Taifa Queens ilimaliza robo ya mwisho ikiongoza kwa 8-7.Katika mashindano hayo ambayo ni ya kwanza kushiriki tangu uongozi mpya wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) ulipoingia madarakani zaidi ya miaka miwili iliyopita, Taifa Queens ilianza kwa kufungwa na Zambia kwa mabao 55-37.Timu hiyo iliyokwenda Botswana kwa ufadhili wa Covenant Bank iliyotoa kiasi cha Sh milioni 40, ilifungwa tena wenyeji Botswana 47-39 kabla ya kupigwa na wachovu Swaziland kwa mabao 47-44 na kumaliza kwa kufungwa na Zimbabwe.Taifa Queens ilifungwa na Zambia mabao 55-37 kabla ya kuchapwa tena na wenyeji Botswana kwa 47-39 na kupigwa 47-44 na Swaziland kabla ya kuhitimisha vipigo kwa kugaragazwa kwa mabao 37-28 na Zimbabwe.
4
MKOA wa Pwani umefanikiwa kukusanya kiasi cha Sh bilioni 147 kutokana na kodi mbalimbali katika kipindi cha miaka minne ya utawala wa Serikali ya Awamu Tano.Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo wakati wa kikao cha mashauriano kati ya wawekezaji na wafanyabiashara wa mkoa huo.Ndikilo amesema kwa kipindi cha mwaka 2011 hadi 2015 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa huo walikusanya kiasi cha Sh bilioni 64.9.“Fedha hizo za kodi zilitokana na kodi za Vat, income tax, paye ukiondoa kodi ya forodha nakushika nafasi ya 12 kati ya mikoa 30 ya kikodi nchini,” amesema Ndikilo.Amesema Mkoa wa Pwani kwa kipindi cha miaka minne iliyopita kwa kigezo cha ukusanyaji wa kodi ulikuwa chini sana na ulikuwa hautajwi lakini katika serikali hii mkoa umepiga hatua kubwa.“Tunaomba kupewa sehemu ya Ranchi ya Taifa Narco ukubwa wa ekari 6,000 kwenye eneo la Bandari Kavu ya Kwala Kibaha Vijijini ili kujenga miundombinu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuegesha magari, biashara, makazi, mahoteli na maghala, viwanda,” amesema Ndikilo.Aidha, alisema Narco wana eneo lenye ukubwa wa ekari 30,000 hivyo endapo watapata eneo hilo ili liwe la uwekezaji kwani ni karibu na Reli ya Kati, Reli ya Kisasa, Reli ya Tazara, sehemu ya kupokea umeme kutoka Bwawa la Nyerere Rufiji, jirani Bandari ya Dar es Salaam, chanzo cha maji ya Dawasa na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Abdala Ndauka amesema changamoto mojawapo ni baadhi ya taasisi za zinazohusika na vibali kutumia nguvu badala ya kutoa elimu.Mfanyabiashara wa viwanda vya kokoto, Ally Murad alisema wanatumia gharama kubwa ya umeme wa jenereta wanaotumia kutokana na kutokuwa na umeme wa Tanesco hivyo wanaomba kupatiwa umeme.
3
WELLINGTON, NEW ZEALAND                  |                       WAZIRI wa Masuala ya Wanawake nchini hapa, Julie Center, ameendesha baiskeli hadi hospitali kujifungua mtoto wake wa kwanza. Genter kutoka Chama cha Kijani, alisema alitumia baiskeli aliyoiendesha mwenyewe baada ya kukosekana nafasi ya kutosha ndani ya gari. Alipiga picha na mumewe wakiwa katika safari hiyo ya kutumia baiskeli na kuiweka katika akaunti yake ya Instagram. Juni mwaka huu, Mbunge Jacinda Ardern, alikuwa mwanasiasa wa pili kujifungulia akiwa kazini na wote yeye na Genter walikua wakihudhuria Clinic pamoja katika hospitali ya umma mjini Auckland. Genter (38) anayejulikana kama shabiki mkubwa wa matumizi ya baiskeli, aliandika katika mtandao wake wa Instagram; “mtuombee baraka, mimi na mwenzangu tumepanda baiskeli kwa sababu hakukuwa na nafasi kwenye gari kutokana na kujaa wasindikizaji.” Waziri huyo atakayechukua miezi mitatu ya likizo ya uzazi, ataungana na baadhi ya wanasiasa waliopata watoto wakati wanatumikia nafasi za kisiasa. Mbunge wa kwanza kupata mtoto akitumikia Bunge la New Zealand, ilikuwa mwaka 1970, huku mwingine akinyonyesha kwa mara ya kwanza katika eneo la kazi mwaka 1983. Nao Austalia walibadilisha kanuni mwaka 2016 kuruhusu watungasheria kuweka sheria ya kunyonyesha katika eneo maalumu ndani ya Bunge. Katika miaka ya hivi karibuni, Sweden, Italia na Bunge la Ulaya wamegusa ulimwengu kwa kupiga kura bungeni wakiwa wamebeba watoto.
2
Na Abdullah Mkeyenge SHUSHA pumzi kwanza. Shusha tena. Tena. Tena. Haya tuendelee. Jana mchana tuliziona picha za Beno Kakolanya akisaini mkataba wa kujiunga na Simba. Msimu ujao atakuwa mchezaji wao. Beno anaenda kukutana na Aishi Salum, Deo Dida. Ni kazi ngumu inayokwenda kumngoja. Mungu amsimamie katika ‘vita’ hii baridi aliyoivaa. Binafsi sikutamani Beno awe mchezaji wa Simba. Nilitamani awe mchezaji wa Azam Fc au timu nyingine, lakini ndani ya Simba amekwenda kupigana vita hivi viwili kwa wakati mmoja. Mungu azidi kumsimamia na hili. Vita vyenyewe si vidogo. Vita vya kwanza ni dhidi yake na Aishi. Hii sio vita ndogo. Ni vita ya kumwagika machozi, jasho na damu. Vita hii wameishindwa wenzake wawili. Dida na Nduda. Wote hawa walibaki kuwa wapenzi watazamaji mbele ya Aishi katika lango la Simba. Ushindani ni kitu kizuri kinachoimarisha kiwango cha mchezaji, lakini ni upinzani upi anaokwenda kukutana nao? Chura anapenda maji, lakini sio ya moto. Mungu azidi kumsimamia na katika hili. Vita ya pili ni dhidi na manazi wa Yanga. Hii ni vita mbaya zaidi kuliko vita ya kwanza. Ubaya wa vita hii ulianzia kwenye mikono ya Kindoki. Maamuzi ya kuondoka katika timu usiyoelewana nayo yanabaki kuwa yako, lakini mfumo aliotumia kuondokea Beno ndiyo uliokwenda kupandikiza chuki vifuani mwa watu wa Yanga. Hii si vita ndogo hata kidogo. Ni vita ngumu kuishinda. Kuna hatua nyingi za nyuma Beno amezipiga tangu alivyoondoka Yanga. Huu ni ukweli mchungu kuumeza. Akiwa na rafiki zake atajiona hajapiga hatua hizo na atajipiga kifua kama dume la nyani, lakini akikaa mwenyewe kujifanyia tathmini atagundua hili. Hayuko Misri na Stars. Amekosa Mil 10 za Makonda. Amekosa kiwanja cha Rais Magufuli. Kibaya kabisa amekosa heshima ya kuwa sehemu ya wachezaji walioifanya Stars ifuzu AFCON baada ya miaka 40 kupita. Moja ya Wanafalsafa wa Kigiriki aliwahi kusema kitakachobadili maisha yako sio ndoto unazoziota usiku mnene, bali ni matendo yako unayoyafanya pale unapoamka asubuhi mpaka unaporudi kulala usiku. Maneno haya yanaishi kichwani mwa Beno. Yanazunguka zunguka. Kila anapokwenda yanamfuata kwa nyuma. Ni kama kivuli. Kwa jinsi alivyoondoka Yanga, Beno alipaswa kwenda katika timu ambayo ingempa utulivu katika kufanya kazi. Huko kwingine angefanya kazi zake vyema katika ukimya mzuri, lakini kutoka Mtaa wa Twiga na kuhamia Mtaa wa Msimbazi kama alivyofanya amekwenda kuishi maisha magumu kinafsi. Asipojiangalia nafasi yake ya kuitwa Stars tena na tena itakuwa shakani. Mungu asiache kumsimamia na katika hili. Hata kimaendeleo na ujenzi wa Stars imara ilipaswa tumuone Aishi na Beno wanakuwa timu tofauti. Huyu anachumia huku, yule anachumia kule, lakini wote kuwa sehemu moja ni lazima mmoja afifie kiwango. Hili lazima liende kutokea. Muda huu ambao Beno amekuwa mchezaji wa Simba na akiwaacha vinywa wazi Yanga, niendelee kumtakia kila la kheri katika changamoto mpya anayokwenda kukutana nayo. Ni Mungu pekee anayejua kilicho mbele, si mwanadamu yeyote.
4
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) limeelezea kupokea kwa masikitiko taarifa za mchezaji wa Simba, Mwinyi Kazimoto, kumpiga na kumshambulia mwandishi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Mwanahiba Richard na kulaani vikali kitendo hicho. TEF imeutaka uongozi wa klabu ya soka ya Simba na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuchukua hatua stahiki za kinidhamu dhidi ya mchezaji huyo kutokana na kitendo alichomfanyia mwandishi huyo akiwa kazini kwani huo ni ukiukwaji wa haki ya kufanya kazi kwa uhuru bila kubughudhiwa na kupigwa. Inadaiwa kuwa Februari 10, mwaka huu Kazimoto alimpiga na kumuumiza mwandishi huyo katika Uwanja wa Kambarage, Shinyanga wakati akitimiza wajibu wake wa kukusanya habari. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa TEF, Theophil Makunga, imeeleza kuwa mchezaji huyo alitumia ngumi na makofi kutimiza uovu wake dhidi ya Mwanaiba huku akimtuhumu kwamba aliwahi kumuandika vibaya gazetini. Taarifa hiyo ilieleza kwa kuwa tukio hilo limeshafunguliwa jalada polisi mjini Shinyanga, TEF inatarajia kwamba Jeshi la Polisi nchini litalichukulia kwa uzito ili mtuhumiwa afikishwe kwenye vyombo vya sheria kujibu mashtaka ya kumshambulia mwandishi huyo na kumjeruhi. “Tunaliomba Jeshi la Polisi litekeleze wajibu wake katika suala hili kwa ukamilifu na kwa hali, tunatoa rai kwa wanamichezo na umma kwa ujumla kwamba kama kuna malalamiko yoyote ya kutokutendewa haki na vyombo vya habari au mwandishi mmoja mmoja ni vyema hatua stahiki zikachukuliwa kama jamii iliyostarabika inavyofanya “TEF kama mdau muhimu kwenye tasnia ya habari haiwezi kufumba macho na kubariki udhalilishaji kama huu, hivyo tunalaani kitendo cha Kazimoto kumpiga na kumjeruhi Mwanaiba,” ilieleza taarifa hiyo.
4
Aveline Kitomary, Dar es salaam MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Rashid Mfaume, ametoa wito kwa wananchi hususani wa Jiji la Dar es Salaam, kutobwete badala yake waendelea kuchukua tahadhari ili kujikinga na virusi vya corona.  Dk  Mfaume alitoa wito huo jana, wakati akipokea msaada wa barakoa 17,500 na vipukusi (sanitizers) lita 700 -kutoka kwa Shirika lisilo la kiserikali la Medipeace linalohusika na mradi wa mama na mtoto katika Mkoa wa Dar es Salaam.  “Licha ya elimu tunayoendelea kutoa juu ya namna ya kujikinga na maambukizi ya corona, tunawahamasisha wananchi wasibweteke katika kipindi hiki, ili kuumaliza kabisa ugonjwa huu katika nchi yetu na hili linawezekana kabisa,” alisema Dk Mfaume.  Alisema msaada uliotolewa utaelekezwa katika vituo vya vya Sinza Hospitali, Vijibweni Hospitali, Rangi Tatu Hospitali, Kituo cha afya Kimara, Kituo cha afya Tandale, Kituo cha afya Mbezi, Kituo cha afya Round table, Kituo cha afya Kimbiji, Kituo cha afya Buguruni, Tegeta Dispensari, Bunju Dispensari. Alisema kumekuwa na ongezeko la wagonjwa katika vituo vya kutolea huduma za Afya, hususan katika Jiji la Dar es Salaam baada ya Serikali kuziteua baadhi ya hospitali kuwa vituo vya kutolea huduma kwa wagonjwa wa Covid-19, hivyo kuelekezwa msaada huo katika vituo vya afya kutasaidia mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya corona.  “Sasa hivi tumeona wagonjwa wameongezeka sana katika vituo vya kutolea huduma za afya, mfano katika Mkoa wa Dar es Salaam baada ya Serikali kuitangaza Hospitali ya Amana kuwa kituo cha kuhudumia wagonjwa wa COVID-19, wagonjwa wengi wamekuwa wakienda katika vituo vingine, hivo msaada huu utasaidia sana kupambana dhidi ya maambukizi mapya,” alisema.  Dk  Mfaume aliwataka wadau wengine kutoka mashirika mbalimbali nchini kuendelea kuisaidia Serikali vifaa kinga dhidi ya corona ili kuvisaidia vituo vya kutolea huduma za afya viweze kujitosheleza mahitaji hayo, hasa kutokana na vituo vya afya kuwa sehemu inayopokea watu tofauti kwa wingi.  Hata hivyo alisema hali ya afya katika Mkoa wa Dar es Salaam ni shwari, huku akisisitiza kuwa Serikali inaendelea kuchukua tahadhari za karibu dhidi ya maambukizi hayo ili kuumaliza kabisa ugonjwa huo nchini.  Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Medipeace Tanzania  Sukyung Kim, alisema shirika hilo linalofadhiliwa na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea ya Kusini (Koica), limekuwa likishirikiana na Wizara ya Afya na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto katika Mkoa wa Dar es salaam. Alisema kutokana na mlipuko wa corona, shirika hilo linaunga mkono juhudi za Serikali za kupambana corona kwa kutoa vifaa kinga ambavyo vitasaidia watoa huduma za afya na wagonjwa wataofika kupata matibabu katika vituo hivyo. 
3
KUTOKANA na umuhimu wa sekta ya elimu na afya, taasisi na mashirika mbalimbali yamekuwa yakijitolea kusaidia sekta hizo. Kwa kuzingatia hilo, Benki ya NMB imetoa zaidi ya Sh milioni 900 katika kipindi cha mwaka huu kwa ajili ya elimu na afya.Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu, Straton Chilongola alisema benki ya NMB kwa mwaka 2019 imetenga Sh bilioni moja kwa jamii, kwa kuzilenga sekta hizo. Kwamba inafanya hivyo ili kuunga mkono juhudi za serikali.Alisema kuwa fedha hizo hutumika kutoa misaada ya vifaa vya ujenzi, madawati, meza, viti na kompyuta. Kwamba NMB hutoa fedha hizo kupitia Kitengo cha Masuala ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR). Chilongola alisema kuna mambo mengi NMB wamepanga kuifanyia jamii, lakini wameamua kuanza na elimu na afya kwa sababu ni mambo waliyoyapa kipaumbele cha kwanza kwani yanagusa jamii moja kwa moja.Alisema kuwa hivi karibuni NMB ilitoa msaada wa madawati 100 kwa shule za msingi za Maduma na Uhambila Kata ya Maduma wilayani Mufindi.“Kwa miaka kadhaa sasa Benki ya NMB tumekuwa mstari wa mbele kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yetu kwa jamii na kwa zaidi ya miaka saba mfululizo tumechangia asilimia moja ya faida yetu kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayotuzunguka,” alisema.Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Jamhuri William akiwakilishwa na Katibu Tarafa wa Malangali, Andrew Chunga katika hafla hiyo, ambapo aliishukuru NMB kwa kusaidia sekta ya elimu. Alitoa mwito kwa benki hiyo kuendelea kutoa misaada mbalimbali katika sekta nyingine zinazokabiliwa na changamoto kubwa.Alisema msaada huo umekuja kwa wakati muafaka kwani shule hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi, zikiwemo barabara, maabara na dawa kwa ajili ya wanafunzi. Alitoa mwito kwa NMB kuendelea kuisaidia shule hiyo na nyingine katika wilaya ya Mafinga. Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ameishukuru benki hiyo kwa msaada wa meza na viti vyenye thamani ya Sh milioni 10 kwa Shule ya Sekondari ya Mrisho Gambo katika Kata ya Mashono Vijijini.Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Aikansia Muro alisema msaada huo ni sehemu ya mchango wao kwa jamii na kuunga mkono juhudi za serikali kuleta maendeleo. Kwamba NMB imejikita zaidi kwenye miradi ya elimu na afya na kusaidia majanga yanayoipata nchi yetu. Alisema benki hiyo ndiyo inayoongoza nchini kwa kuwa na matawi 229, ATM zaidi ya 800, NMB Wakala zaidi ya 6,000 na wateja zaidi ya milioni tatu, idadi ambayo ni kubwa ukilinganisha na benki nyingine nchini.Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Rorya mkoani Mara, Simon Chacha amepokea msaada wa madawati 125 kwa ajili ya shule za msingi Minigo na Ryaghati wilayani Rorya. Chacha alisema kuwa NMB imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo wilayani humo na aliahidi kuendeleza ushirikiano na uhusiano huo.Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, Amos Mubusi alisema benki hiyo ilipokea maombi ya msaada kwa shule hizo na kuyafanyia kazi kwa haraka.“Vitu vyote hivi tunavyokabidhi leo kwa shule hizi vina thamani ya Sh milioni 15 na ni sehemu ya misaada ambayo benki tunatoa kwa ajili ya maendeleo ya jamii,” alisema Mubusi.
3
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma, imepanga kuanza kutoa elimu kwa umma ya kujiepusha, kujihadhari na kuzuia vitendo vya rushwa katika Uchaguzi Mkuu ukaofanyika mwishoni mwa mwaka huu 2020.Akizungumza na vyombo vya habari mwishoni mwa wiki, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, Sosthenes Kibwengo alisema mkakati huo wa uelimishaji umma ,upo ndani ya mikakati ya robo ya kwanza ya Januari hadi Machi mwaka 2020.Kibwengo alisema katika robo hiyo ya kwanza, taasisi hiyo imejipanga kukusanya taarifa mbalimbali kuhusu vitendo vya rushwa na kupambana na wale wote, watakaotumia rushwa katika kutafuta uongozi katika uchaguzi.“Yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo vya rushwa kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu ujao, Takukuru itapambana naye,” alisema.Kibwengo alisema katika robo hiyo, pia taasisi hiyo itaendelea kutekeleza majukumu ya kuelimisha umma yaliyokuwa yakitekelezwa katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka Oktoba hadi Desemba 2019.Alisema Takukuru itaendelea na kuhamasisha jamii, kushiriki kivitendo katika kukemea na kuzuia vitendo vya rushwa katika maeneo mbalimbali, hasa wakati wa uchaguzi mkuu ujao.Alisema katika kipindi hicho, Takukuru iliweka mkazo kuzuia vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka jana, hivyo katika mwaka huu itaendelea kuweka mkazo katika kuzuia vitendo hivyo wakati wa uchuguzi mkuu.Pia itaendelea na ‘Kampeni yaVunja Ukimya, Kataa Rushwa ya Ngono’ pamoja na ‘Kampeni ya Utatu’, inayopinga vitendo vya rushwa katika maeneo mbalimbali, yakiwemo rushwa kwa askari wa usalama barabarani (trafiki). Alisema katika kipindi cha Oktoba hadi Desemba mwaka jana, Takukuru ilirusha vipindi zaidi ya 43 kwenye redio na televisheni, vya kuelimisha jamii kujihadhari na vitendo hivyo.Pia ilifanya mikutano ya hadhara 84 na semina 89 kwa ajili ya kuelimisha makundi mbalimbali ya jamii wakiwemo wananchi wa kawaida, wanasiasa, wanafunzi, watumishi wa umma na sekta binafsi.Alisema katika kipindi hicho, pia Takukuru ilikazia makuzi ya maadili mema kwa vijana, ambapo klabu 103 za wapinga rushwa katika shule za msingi, sekondari na vyuo ziliundwa.Pia katika kipindi hicho, klabu 122 ambazo zilikuwa tayari zimekwishaundwa, zilitembelewa na viongozi wa taasisi hiyo kwa ajili ya kuziimarisha. Kibwengo alisema katika kupambana na rushwa katika robo hiyo, pia Takukuru ilikamilisha uchunguzi wa majalada 14 na kufungua kesi saba, zilizohusu viongozi wa vyama vya akiba na mikopo, watumishi wa halmashauri na watu binafsi.Ilipokea malalamiko 147 kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu vitendo vya rushwa na makosa yanayohusiana na vitendo hivyo, mengi kati yake yakiwa kutoka ardhi kwa asilimia 31.4. “Taasisi nyingine zilizolalamikiwa ni serikali za mitaa kwa asilimia 22.9, polisi (14.3), vyama vya siasa (11.4) mahakama (4.3), elimu (4.3) na sekta zilizosalia (11.4)” alisema.
3
Aidha kocha huyo amekuwa na wasiwasi na kocha wa Yanga, Hans van Pluijm kwamba atampa kocha Charles Mkwasa mbinu za kuiua Nigeria. Taifa Stars kesho itaikaribisha Nigeria kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam katika mechi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2017.Akikaririwa kwenye mtandao wa Supersport jana, Oliseh alisema amekuwa akifuatilia mikanda mbalimbali ya video za michezo ya Stars, lakini amekuwa gizani kuifahamu vizuri timu hiyo.Oliseh alikiri kwamba yeye na makachero wake hawajaiona mikanda ya mechi za Stars chini ya kocha mpya Mkwasa na hivyo wako gizani kwani hawafahamu Stars itaingia vipi uwanjani kesho.Oliseh aliyasema hayo akiwa Abuja juzi: “Tanzania ni timu isiyotabirika na kwa maana hiyo tunaweza kupata mshangao katika mechi hiyo kwa sababu hatufahamu falsafa ya kocha mpya na wanacheza nyumbani,” alisema.Kitu kimoja ambacho Oliseh ana uhakika nacho ni kwamba Mkwasa atakuwa amepewa mbinu nakocha Mkuu wa Yanga Hans van Der Pluijm. Mkwasa ni msaidizi wa Van Pluijm Yanga.Pluijm aliyewahi kufanya kazi Ghana katika klabu za Kotoko na Chelsea Berkum anaifahamu soka ya Afrika Magharibi na hakuna ubishi kwamba atakuwa na mbinu kadhaa alizowekeza kwa Mkwasa.Kambi ya Nigeria imeingia hitilafu kwani licha ya kuondoka kwa Joel Obi kutokana na kuwa majeruhi, nahodha wa timu hiyo Enyama amefiwa na mama yake. Stars ilikuwa Uturuki kwa kambi ya wiki moja na ilirejea nchini juzi tayari kwa mechi hiyo.Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mkwasa aliliambia gazeti hili kuwa wanaifahamu Nigeria ni timu kubwa lakini hawaiogopi na wako tayari kukutana nayo. “Tunashukuru tumefika sala nyumbani na tupo tayari kwa ajili ya mechi ya Jumamosi (kesho)…Ninachoweza kusema ni kwamba wapinzani wetu tunawafahamu na wanafahamika kutokana na uwepo wao wa mara kwa mara kwenye michuano ya kimataifa, lakini mimi na timu yangu hatuliogopi hilo, tutakachokifanya ni kupambana nao mwanzo mpaka mwisho,” alisema.Stars inaingia uwanjani kesho ikitoka kufungwa mabao 3-0 dhidi ya Misri huku wapinzani wake Nigeria wakitoka kushinda mabao 2-0 dhidi ya Chad katika mechi zilizochezwa Juni mwaka huu.Kwa mujibu wa viwango vya ubora wa Fifa vilivyotolewa jana, Tanzania imeachwa na Nigeria kwa nafasi 87 ikishika nafasi ya 140 huku wapinzani wao wakiwa kwenye nafasi ya 53.
4